Kiswahili: translationNotes Print

Updated ? hours ago # views See on WACS

Leviticus 1

Leviticus 1:1

Yahweh

Hili ndilo jina la Mungu ambalo alilifunua kwa watu wake katika Agano la Kale.

kutoka kweye hema la kukutania, akisema, "Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, 'Mtu yeyote

Hapa Yahweh anaanza kuzungumza na Musa. Hotuba hii inamalizikia katika 3:17. Hii inaweza kufasiriwa bila nukuu ndani ya nukuu. :"Kutoka kwenye hema la kukutania na akamwambia Musa kuzungumza na watu wa Israeli: 'Mtu yeyote aletapo"

'Mtu yeyote kutoka miongoni mwenu

"mmoja wenu yeyote" au "yeyote wa kwenu"

Leviticus 1:3

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendele kumwambia Musa yawapasayo watu wa Israeli kufsny ili kwa mba sadaka zao zitakuwa zenye kubalika kwa Yahweh.

.Iwapo toleo lake ... naye itambidi kutoa

Hapa "yake" na "naye" humaanisha mtu aletaye sadaka kwa Yahweh. laweza kufasiriwa katika nafsi ya pili kama lilivyo katika 1:1 : iwapo toleo lako...yapasa utoe

ili iweze kukubalika mbele za Yahweh

Hili linaweza kufasiriwa katika muundo tendaji: :Ili kwamba Yahweh aikubali"

Ataweka mikono yake

Hiki ni kitendo cha kiishara kinachomfananisha mtu na mnyama anayemtoa. Katika njia hii mtu anajitoa mwenyewe kwa Yahweh kwa kupitia mnyama, ili kwamba Mungu atasamehe dahambi za mtu huyo wanapomuua mnyama.

ndipo itakuwa imekubalika badala yake ili kufanya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe

Hii inaweza kufasiriwa katika muundo tendaji: "Kisha Yahweh ataikubali machini pake na kuzisamehe dhambi zake"

Leviticus 1:5

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa watu wanachotakiwa kufanya.

Naye yampasa kumchinja huyo fahali

Hapa "naye" humaanisha yule anayetoa hiyo sadaka. linaweza kutamkwa katika nafsi ya pili. : "Nawe yakupasa kumchinja huyo fahali"

mbele za Yahweh

"Katika uwepo wa Yahweh"

wataileta hiyo damu

Inadokeza kwamba makuhani wangeikinga damu kwenye bakuli ilipotiririka kutoka kwa mnyama. Kisha wangelileta hillo bakuli lenye damu ndani yake na kuliwasilisha kwaYahweh kwenye madhabahu.

Kisha ataichuna ngozi hiyo sadaka ya kuteketezwa na kuikatakata vipande.

Kama ilivyoonyeshwa kwenye 1:9, Mtu alilazimiika pia kuosha matumbo na miguu ya mnyama kwenye maji. Mhisika mwenyewe alilazimika kufanya hivyo kabla hajawapa makuhani vile vipande ili kwamba wangeweza kuviweka juu ya madhabahu. Unaweza kuyatamka hayo maelekeza kuwa yalikuwa ni matumbo na miguu.

Naye ataichuna ngozi

Hapa neno "naye" humaanisha yule anayetoa hiyo sadaka.

Leviticus 1:7

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa kiwapasacho watu kutenda ili matoleo yatakubalika kwa kwake.

wataweka moto juu ya madhabahu na kuweka kuni ili kuuchochea huo moto

Hili laweza kumaanisha kwamba makuhani mkaa wa moto juu ya madhabahu, kisha wakaweka kuni juu ya mkaa. : wataweka kunu juu ya madhabahu na kuwasha moto"

kuuchochea huo moto

Hii ni nahau inayomaanisha kuendelea kuweka kuni kwenye moto. Moto juu ya madhabahu nilazima uendelee kuwaka bila kuzimika

Lakini matumbo yake na miguu ataiosha kwa maji

Mtu huyo angefanya hivi kabla hajavitoa vipande kwa makuhani waviweke juu moto. U naweza kutamka hivi mwishoni mwa 1:5

Mtumbo

Ni hilo tumbo na utumbo

naye ataiosha

Hapa neno "naye" humaanisha anayetoa hiyo sadaka.

nayo italeta harufu ya kupendeza kwangu

Yahweh akiwa amependezwa na utoaji dhabihu wa dhati wa aabuduye unamezungumziwa kana kwamba Yahweh alikuwa amependezwa na harufu nzuri ya dhabihu.

sadaka iliyofanywa kwangu kwa moto.

Yahweh anamwambia Musa kwamba ni lazima matoleo yawe yanachomwa kwa moto. Hili laweza kutamkwa katika muundo tendaji. : "sadaka ya kuteketezwa kwangu"

Leviticus 1:10

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa liwapasalo watu kutenda

mbele za Yahweh

"katika uwepo wa Yahweh"

Leviticus 1:12

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa liwapasalo watu kutenda

Naye ataikata...iliyofanywa Kwake kwa moto.

Ajili ya 1:12-13, tazama 1:7 ili uone wingi wa maneno haya yalivyofasiriwa

Naye ataikata

Hapa neno "naye" humaanisha mtu anayetoa dhabihu. Laweza kufasiriwa katika nafsi ya pili. :"Nawe utaikata"

italeta harufu ya kupendeza kwa Yahweh

Yahweh akiwa amependezwa na utoaji dhabihu wa dhati wa aabuduye unamezungumziwa kana kwamba Yahweh alikuwa amependezwa na harufu nzuri ya dhabihu.

itakuwa sadaka ya iliyofanywa...kwa moto.

Yahweh anamwambia Musa kwamba ni lazima makuhani wazichome sadaka zao kwa moto. Sentensi hii inaweza kufasiriwa kwenye muundo tendaji. :"itakuwa sadaka ya kuteketezwa kwangu" au "itakuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Yahweh"

Leviticus 1:14

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa kiwapasacho watu kutenda

nyonga shingo na kukinyoa kichwa chake,

popotoa/songonyoa kichwa chake na kuking'oa kutoka mwilini

Kisha damu yake itachuruzishwa

Sentensi hii yaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji: "Kisha itampasa kuhani kuichuruzisha damu yake"

Leviticus 1:16

Ni lazima akiondoe

"Ni lazima kuhani"

kibofu chake pamoja na uchafu wake

Kibofu ni kwenye koromeo la ndege mahali ambapo chakula ambacho hakijameng'enywa hutunzwa.

nacho atakitupa...kando ya madhabahu

Neno "nacho" hapa humaanisha kibofu pamoja na uchafu wake

italeta harufu ya kupendeza kwa Yahweh

Yahweh akiwa amependezwa na utoaji dhabihu wa dhati wa aabuduye unazungumziwa kana kwamba Yahweh alikuwa amependezwa na harufu nzuri ya dhabihu. Tazama lilivyotafsiriwa hili katika 1:7

nayo itakuwa sadaka iliyofanywa Kwake kwa moto.

Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "itakuwa sadaka ya kuteketezwa kwangu" au "itakuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Yahweh"

Leviticus 2

Leviticus 2:1

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kumbia Musa liwapasalo watu kutenda.

liwe unga safi

"Iiwe unga safi kabisa" au "uwe unga uliobora"

unga

ngano ilinyosagwa

Itampasa kuipeleka

itampasa kuuchukua

atatwaa konzi

"atachukua unga anaoweza kuubeba mkononi mwake

sadaka ya kuwakilisha

konzi ya sadaka ya nafaka huwakilisha sadakanzima ya nafaka. Hii inamaanisha kwamba sadaka nzima ni ya Mungu.

Nayo itatoa harufu nzuri ya kupendeza kwa Yahweh.

Yahweh akiwa amependezwa na utoaji dhabihu wa dhati wa aabuduye unazungumziwa kana kwamba Yahweh alikuwa amependezwa na harufu nzuri ya dhabihu. Tazama lilivyotafsiriwa katika 1:7

Ni kitakatifu sana kwa Yahweh kutoka kwenye sadaka iliyofanywe kwa Yahweh kwa moto.

Hili laweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. : "itakuwa sadaka ya kuteketezwa Kwake"

Leviticus 2:4

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa kwamba watu hao pamoja na makuhani yawapasa wafanye hivyo ili sadaka zao ziweze kukubalika kwake.

uliookwa kweye tanuru

Sentensi hii yaweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "uliouoka kwenye tanuru"

tanuru

Huenda hiki kilikuwa ni chombo kilichotengenezwa kwa udongo chenye uwazi shimo katikati. Moto uliwashwa chini ya tanuru, na joto lingeoka donge la unga ndani ya tanuru.

mkate laini wa unga safi

yaeleweka kwamba mkate laini haukuwa na hamira.

uliopakwa mafuta

Tafsiri kirai hiki kuonesha kwamba mafuta ni lazima yapakwe kwenye mkate. :"pamoja na mafuta juu ya mkate"

Iwapo toleo lako la nafaka limeokwa kwa kikaango cha chuma

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : Iwapo unaioka sadaka yako ya nafaka katika kiaango cha chuma"

kikaango cha chuma

Hii ni sahani nzito iliyotengenezwa ama kwa udongo au chuma. Sahani iliwekwa juu ya moto, na donge la ungu lilipikwa juu ya sahani.

Leviticus 2:6

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia musa kwamba watu hao na makuhani yawapasa wafanye hivyo ili sadaka zao ziweze kukubalika kwake

utaigawanya

Hapa "inayogawanywa" ni sadaka ya nafaka iliyopikwa kwenye kikaaongo cha chuma.

Iwapo sadaka yako ya nafaka imepikwa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Ikiwa unaipika sadaka yako ya nafaka"

katika sufuria

Sufuria ilikuwa sahani yenye kingo zikiizunguka. Bonde la unga lilidumbuzwa ndani ya sufuria na kupikwa juu ya moto.

lazima iwe imeandaliwa

Yaweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Ni lazima uiandae"

Leviticus 2:8

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia musa kwamba watu hao na makuhani yawapasa wafanye hivyo ili sadaka zao ziweze kukubalika kwake

ililofanywa kwa vitu hivi

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. : "ulioutengeneza kutokana na unga na mafuta"

nayo itawasilishwa

Yaweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Utaiwasilisha"

Ndipo kuhani... ifanywayo kwa moto.

Kwa ajili ya2:9-10 tazama maelezo ya sura ya 2:1

sadaka ya kuwakilisha

Tazama maelezo ya sura ya 2:1

Itakuwa sadaka kuiliyofanywa kwa moto

Hii inaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. : "Itakuwa sadaka ya kuiteketeza"

italeta harufu ya kupendeza kwa Yahweh

Tazama maelezo ya sura 1:7

kutoka kwenye sadaka ifanywayo kwa Yahweh kwa moto

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. : "kutoka kwenye sadaka ya kuiteketeza kwa Yahweh"

Leviticus 2:11

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa kwamba watu hao na makuhani yawapasa wafanye hivyo ili sadaka zao ziweze kukubalika kwake

Hakutakuwa na sadaka ya nafaka utoayo kwa Yahweh itakayofanyizwa kwa hamira

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. : "Usitumie hamira kwenye sadaka ya nafaka uitoayo kwa Yahweh"

kuwa sadaka ifanywayo kwa moto

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. : "kuwa sadaka ya kuteketeza

Nawe utazitoa

"Nawe utazitoa sadaka za nafaka zilizo na hamira au asali"

hazitatumika kuleta harufu ya kupendeza itolewayo juu ya madhabahu

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. ; "utazitumia kuleta harufu ya kupendeaza juu ya madhabahu" au "hutaziteketeza juu ya madhabu"

chumvi ya agano la Mungu wako

Huashiria kwamba chumvi ni ishara inayowakilisha agano la Mungu.

Leviticus 2:14

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa kwamba watu hao na makuhani yawapasa wafanye hivyo ili sadaka zao ziweze kukubalika kwake

iliyobanikwa kenye moto, na kupondwa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. : "Ile uliyoipika kwenye moto na kisha kusagwa"

sadaka ya kuwakilisha

Tazama maelezo katika sura ya 2:1

Hii ni sadaka ifanywayo kwa Yahweh kwa moto.

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. : "Hii ni sadaka ya kutekezwa kwa Yahweh"

Leviticus 3

Leviticus 3:1

Taarifa kwa ujumla

Musa anaendelea kuwaambia watu kile ambacho Yahweh anataka wao wafanye.

mbele za Yahweh

"katika uwepo wa Yahweh" au "kwa Yahweh"

Ataweka mikono yake

Hili ni tendo la kiishara ambalo humfananisha mtu na mnyama anayemtoa. Katika njia hii mtu huyo anajitoa mwenyewe kwa Yahweh kwa kupitia mnyama. Tazama lilivyotafsiriwa katika sura ya 1:3

wana wa Aroni watainyunyiza damu yake

Inaashiria kwamba kabla hawajainyunyiza damu ,waliikinga kwanza hiyo damu katika bakuli walipokuwa akiichuruzisha kutoka kwa Munyama.

Leviticus 3:3

Matumbo

Hili ni tumbo na utumbo

ya kiununi

Hii ni sehemu ya mwili wa mnyama kwenye maeneo ya ndani ya uti wa mgongo kati ya mbavu na mfupa wa nyonga.

kitambi cha ini

Hii ni sehemu ya ini iliyojikunja au kulizunguka. Sehemu hii huonekana kuwa ni sehemu ya ini iliyobora kabisa kwa kula. : "Sehemu ya ini iliyobora"

Hii italeta harufu ya kupendeza mbele za Yahweh

Tazama ufafanuzi uliotolewa katika sura ya 1:7

itakuwa sadaka itolewayo Kwake kwa moto.

Hili laweza kutafsiriwa katika mtindo tendaji. : "nayo itakuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Yahweh"

Leviticus 3:6

amtoe mbele za Yahweh

"amtoe mkatika uwepo wa Yahweh" au "amte kwa Yahweh"

Ataweka mkono wake juu ya kichwa

Hili ni tendo la kiishara ambalo humfananisha mtu na mnyama anayemtoa. Kwa njia hii mtu huyo atakuwa anajitoa mwenyewe kwa Yahweh kupitia mnyama.

wana wa Aroni watanyunyiza damu

Inaashiria kwamba kabla hawajanyunyiza hiyo damu, waliikinga kwanza kwenye bakuli ilipokuwa inachuruzika kutoka kwa mnyama

Leviticus 3:9

sadaka ifanywayo kwa moto

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "kuwa sadaka ya kuteketezwa"

Yale mafuta, mafuta yote...na hizo figo —ataiondoa hii yote.

Lile tamko "ataiondoa hii yote" laweza kuwekwa mwanzoni mwa sentensi. : "Atayaondoa mafuta, hayo mafuta yote...hizo figo"

matumbo

Sehemu hizi ni tumbo na utumbo.

yaliyo karibu na matumbo, na figo zote mbili

Sentensi mpya yaweza kuanzia hapa. : "iliyo karibu na mbatumbo. Ni lazima ataziondoa hizo figo"

karibu na kiuno

Hii ni sehemu ya mwiili kwenye sehemu ndani ya uti kati ya mbavu na mfupa wa nyonga.

kitambi cha ini

Hii ni sehemu ya ini yenyekupinda au kulizunguka. Sehemu hii huonekana kuwa bora sana kwa kula. : "ile sehemu ya ini iliyobora kabisa"

ataiteketeza yote juu ya madhabahu kuwa sadaka ya chakula ya kuteketezwa kwa Yahweh

Hapa haikukusudiwa kumaanisha kwamba Yahweh hula chakula. : "ataviteketeza vitu hivyo juu ya madhabahu viwe sadaka kwa Yahweh. Vitu hivyo vitatokana na mazao yako ya chakula"

Leviticus 3:12

mbele za Yahweh

"katika uwepo wa Yahweh" au "kwa Yahweh"

Ataweka mikono yake juu ya kichw

Hili ni tendo la kiishara ambalo humfananisha mtu na mnyama anayemtoa. Kwa njia hii mtu huyo atakuwa anajitoa mwenyewe kwa Yahweh kupitia mnyama.Tazama maelezo katika 1:3

wana wa Aroni watainyunyiza damu yake

Inaashiria kwamba kabla hawajainyunyiza hiyo damu, waliikinga kwanza kwenye bakuli ilipokuwa ikichuruzika kutoka kwa mnyama.

atatoa dhabihu yake iliyofanywa kwa mot

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "ataitoa sdhabihu yake kwa moto" au "ataichoma dhabihu yake"

Leviticus 3:15

Naye ataziondoa pia

Neno "naye" hapa humaanisha mtu anayetoa dhabihu.

ataiteketeza hiyo yote juu ya madhabahu kuwa matoleo ya chakula ya kuteketezwa

Hapa haikukusudiwa kumaanisha kwamba Yahweh hula chakula. : "ataviteketeza vitu hivyo juu ya madhabahu viwe sadaka kwa Yahweh. Kitakuwa ni chakula chao alichopwa Yahweh"

kutoa harufu ya kupendeza

Yahweh hupendezwa na harufu ya nyama iliyochomwa anapopendezwa na usafi wa aabuduye. Tazama lilivyotafsiriwa katika 1:7

Itakuwa ni amri ya kudumu kwa vizazi vya watu wako

Hii humaanisha kwamba wao pamoja na vizazi vyao lazima waitii amri hii.

au damu

"au kutumia damu"

Leviticus 4

Leviticus 4:1

Yahweh akazungumza na Musa akisema, "Waambie watu wa Israeli, 'mtu yeyote atendapo dhambi

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Nukuu halisi yaweza kutamkwa kama nukuu taarifa iliyotajwa. : Yahweh akazungumza na Musa na akamwambia awaambie watu wa Israeli hivi: 'Mtu yeyote atendapo dhambi"

ambayo Yahweh ameagiza yasitendwe

Hili laweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. : "Ambayo Yahweh amewaamru watu wastende"

endapo anafanya jambo fulani lililokatazwa,

Hili laweza kufasriwa katika mtindo tendaji. : "iwapo anafanya jambo ambalo Yahweh aliruhusu"

yafuatayo lazima yafanyike

Hiii yaaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. : "yapasa afanye yafuatayo"

na kuleta hatia juu ya watu

Ile nomono dhahania "hatia" yaweza kutamkwa kama kivumishi. : "kwa kiasi cha kusababisha watu kujisikia wenye hatia"

Leviticus 4:4

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa kiwapasacho watu kutenda.

Atamleta huyo fahali

"Kuhani atamleta huyo fahali"

ataweka mikono yake juu ya kichwa chake

Tazama maelezo ya sura 1:3 uone lilifasiriwa.

Kuhani mpakwa mafuta atachukua sehemu ya damu

Inaonyesha kwamba kuhani aliikinga kwanza damu kwenye bakuli ilipokuwa inachuruzika kutoka kwa huyo mnyama.

Leviticus 4:6

kuinyunyiza

"kutiririsha sehemu yake" au "kudondosha sehemu yake"

pembe za madhabahu

hii humaanisha kwenye kona za madhabahu. Zimesongoka kama pembe za makisai. : "Michomozo iliyo kwenye kona za madhabahu"

ataimwaga chini

"ataitupa nje damu iliyobaki"

kwenye kitako cha madhabahu

chini ya madhabahu

Leviticus 4:8

Naye atayakata

"Kuhani atayakata"

yale mafuta yanayofunika matumbo. ..pamoja na figo—ataikata hii yote

Yale maelezo "ataikata hii yote" yaweza kuwekwa mwanzoni mwa sentensi. : "Atayakata mafuta yote yafunikayo matumbo...pamoja na hizo figo"

matumbo.

Haya ni tumbo na utumbo

karibu na kiuno

Hii ni sehemu ya mwili juu ya upande wa ndani wa uti wa mgongo kati ya mbavu na mfupa wa nyonga.

kitambi cha in

Hii ni sehemu ya ini iliyojikunja au kulizunguka. Sehemu hii huonekana kuwa ni sehemu ya ini iliyobora kabisa kwa kula. : "Sehemu ya ini iliyobora"

Leviticus 4:11

Ngozi ... mabaki yoyote ya nyama, atazipeleka hizo zote nje

Yale maelezo "atazipeleka hizi zote" Yaweza kuweka mwanzoni mwa sentensi. : "Kuhani atapeleka nje hiyo ngozi..mabaki ya fahali"

eneo ambalo wamelisafisha kwa ajili yangu

Eneo kuwa safi kiibada na pa kufaa kutumia katika kumtumikia Mungu linasemwa kuwa lilikuwa safi kimaumbile.

wamelisafisha kwa ajili yangu

"Wamelisafisha" hapa humaanisha hao makuhani na "Mimi" humaanisha Yahweh.

Leviticus 4:13

bila kukusudia

"bila kujua"

ameamru yasitendwe

Hili laweza kuutamkwa katika mtindo tendaji. : "alichowaamru wasikitende"

hiyo dhambi waliyoitenda ikawa imejulikana

Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "wanapotambua kwamba wametenda dhambi"

wataweka mikono yao juu ya kichwa

Tazama maelezo katika sura 1:3 uone lilivyofasiriwa

huyo fahali atachinjwa

Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Nao watamuua huyo fahali"

Leviticus 4:16

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Munsa yawapasayo watu kutenda.

Kuhani aliyepakwa mafuta ataleta damu

Inamaanisha kwamba huyo kuhani aliikinga damu kwenye bakuli ilipotiririka

mbele ya pazia.

Inamaanisha kwamba hili ni pazia mbele ya patakatifu pa patakatifu

Leviticus 4:18

Ataweka

"Naye kuhani ataweka"

pembe za madhabahu

hii hurejelea kona za madhabahu. Zimechongwa kama pembe za ng'ombe. Tazama lilivyofasiriwa katika Sura ya 4:6

ataimwaga damu yote

Ataimwaga damu iliyosalia

mafuta yote kutoka kwake

"mafuta yote kutoka kwa mnyama na kuyachoma hayo mafuta"

Leviticus 4:20

inavyompasa kumfanyia

"Ni lazima kuhani afanye"

kuhani atawafanyia watu upatanisho

Nomino dhahania "upatanisho" yaweza kama kitenzi. : "Kuhani atapatanisha kwa ajili ya kwa ajili ya dhambi za watu"

nao watakuwa wamesahewa

Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Naye Yahweh atawasamehe wao"

Leviticus 4:22

Yahweh Mungu wake ameamru yasitendwe

hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Mungu amewaamru watu wasitenda"

Nayo dhambi yake aliyoitenda imefahamisha kwake

hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. ; "kisha naye ameshatambua kwamba katenda dhambi"

Leviticus 4:24

Naye ataweka

"Mtawala ataweka"

ataweka mkono wake juu ya kichwa

Tazama lilivyofassiriwa katika sura ya 1:3

mahali ambapo huchinja

"makuhani wanapochinja"

mbele za Yahweh

"katika uwepo wa Yahweh" au kwa Yahweh"

Kuhani ataichukua damu

Inamaanisha kwamba kuhani aliikinga damu kwenye bakuli damu ilipotirirka kutoka kwa mbuzi.

pembe za madhabahu

Tazama maelezo kwenye sura ya 4:6 uone linavyofasiriwa

Leviticus 4:26

Naye atateketeza

"Kuhani atateketeza

Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya mtawala

Ile nomino dhahania "upatanisho"yaweza kutaamkwa kama kitenzi. : "Kuhani atapatanisha kwa ajili ya mtawala"

naye mtawala kulingana

Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Yahweh atasamehe dhambi za mtawala"

Leviticus 4:27

Yahweh amemwamru yeye yasitendwe

Watu wote wa Israeli waliamriwa wasitende dhambi. Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Yahweh aliwaamru watu wasiyatende"

dhambi yake aliyoitenda itakuwa imejulikana kwake

Hili laweza kutmkwa katika mtindo tendaji. : "naye amekuwa na ufahamu juu ya dhambi aliyoitenda.

Leviticus 4:29

Ataweka mkono wake juu ya kichwa

Tazama mafafanuzi katika sura ya 1:3 uone lilivyofasiriwa

Kuhani atachukua kiasi cha damu

Inamaanisha kwamba kuhani aliikinga damu ya kwenye bakuli wakati ilipotiririka kutoka kwa mnyama

pembe za madhabahu

Tazama katika sura ya 4:6 uone lilivyofasiriwa.

Damu yote iliyobaki

Damu yote iliyobaki kwenye bakuli.

Leviticus 4:31

Naye atayakata

"Naye'" hapa humaanisha yule mtu anayetoa sadaka

yanvyokatwa hayo mafuta

Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "ni kama tu vile mtu akatavyo hayo mafuta"

ataiteketeza

"atayachoma mafuta"

ili kuleta harufu ya kupendeza kwa Yahweh

Tazama maelezo yaliyotolewa kwenye sura 1:7 ili uone maneno hayo yalivyofafanuliwa

Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya mtu hyo

Ile nomino dhahania "upatanisho" yaweza kutamkwa kama kitenzi. "Kuhani atapatanisha kwa ajili ya dhambi za mtu huyo"

naye atakuwa amesamehewa.

Hili laweza kutamkwa katika mtingo tendaji. : "Yahweh atazisamehe dhambi za mtu huyo"

Leviticus 4:32

Ataweka mkono juu ya kichwa

Tazama maelezo ya sura ya 1:3 ili kuona lilivyofasiriwa.

mahali wanapochinja s

"mahali makuhani wachinjapo"

Leviticus 4:34

pembe za madhabahu

Tazama maelezo ya sura ya 4:6 ili kuona linavyofasiriwa.

naye ataimwaga damu yake yote

"Naye ataimwaga damu yake yote iliyobaki"

Naye tayakata mafuta

"Naye" hapa humrejelea mtu anayetoa hiyo dhabihu.

kama tu vile yakatwavyo mafuta ya mwana-kondoo

Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "kama tu vile mtu akatavyo hayo mafuta ya Mwana-kondoo"

matoleo ya Yahweh yafanywayo kwa moto

Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Matoleo ya kuteketezwa kwa Yahweh

atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa dhambi aliyoifanya

Ile nomino dhahania "upatanisho" yaweza kutamkwa kama kitenzi. :atapatanisha kwa ajili ya dhambi aliyotenda huyo mtu"

na mtu huyo atakuwa amesahewa.

Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Yahweh atasameha dhambi ya mtu huyo"

Leviticus 5

Leviticus 5:1

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendlea kumwambia Musa yawapasayo watu kutenda

ushahidi fulani kuhusu kile alichotakiwa kushudia

Sheria na viongozi wa kiyahudi viliwataka watu kushuhudia iwapo walikuwa mashahidi kwa uharifu. Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "jambo fulani ambalo hakimu amemtaka yeye kushuhudia"

Mungu amekitaja kuwa ni najisi

Kitu fulani ambacho Mungu amekita kuwa hakiwafai watu kukigusa au kukila kimesemwa kuwa kana kwamba kilikuwa kichafu kwa mwonekano.

mzoga

"maiti"

yeye ni najisi

Mtu asiyekubalika katika makusudi ya Munngu husemwa kana kwamba ni mtu aliyekuwa mchafu kimwili.

Leviticus 5:3

ikiwa agusa unajisi wa mtu fulani, haijalishi ni unajisi wa aina gani

Ile nomino dhahania "unajisi" yaweza kutamkwa kama kivumishi. : "iwapo nagusa kitu chochote ambacho humfanya mtu najisi"

unajisi

Kitu fulani ambacho Yahweh amekitamka kuwa hkifai kwa mtu kukigusa au kukila huzungumziwa kana kwamba kilikuwa najisi kwa monekao.

hakuwa na habari juu yake

"yeye ahitambui" au "hajui juu yake"

anaapa kwa midomo yake

Hapa "midomo" huwakilisha mtu mzima. : "iwapo mtu yeyote anaapa bila kujali"

mtu huapa bila kujali,

Hii humaanisha kuapa kiapo bila kufikiri kwa kumaanisha juu yake. Inamaanisha kwamba baada ya mtu kuwa anaapa kiapo ambacho ama hawezi kukitimiza au hataki hasa kukitimiza.

Leviticus 5:5

Maelezo kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa yawapasayo watu kutenda.

naye kuhani atafanya upatanisho

Ile nomino dhahania "Upatanisho" yaweza kutamkwa kama kitenzi. : "Kuhani atapatanisha kwa ajili yake"

Leviticus 5:7

Iwapo hataweza kununua mwana-kondoo

Iwapo hana fedha ya kutosha kununua mwana-kondoo

naye atamvunja shingo yake lakini ataacha kichwa chake kinaning'inia wala hataiondoa kabisa shingo yake

"naye atamuua kwa kukipindua kichwa chake na kuivunja shingo yake, lakini hatakiondoa hichwa"

Leviticus 5:10

kama ilivyoelezwa kwenye maelekezo

Hii yaweza kutakwa katika mtindo tendaji. : "kama alivyoelekeza Yhweh"

naye kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya dhambi aliyotenda

Ile nomino dhahania "upatanisho" yaweza kutamkwa kama kitenzi. : "Naye kuhani atapatanisha kwa ajili ya dhambi ile ambayo ametenda

naye huyo mtu atakuwa amesamehewa

Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Yahweh atamsamehe mtu huyo"

Leviticus 5:11

sehemu ya kumi ya efa

Efa moja ni sawa sawa na lita 22. Sehemu ya kumi ni kama lita 2 hivi

sehemu ya kumi

Hii ni sehemu moja ya kumi zilizo sawa

Leviticus 5:12

Naye atauleta

"Naye yampasa kuleta unga safi"

sadaka ya kuwakilisha

konzi kuhani chomayo juu ya madhabahu huwakakilisha matoleo yote. Hii humaanisha matoleo yote ni ya Yahweh, tazama sura ya 2:1

atafanya upatanisho

Ile nomino dhahania "upatanisho" yaweza kutamkwa kama tendo. : "atamatanisha"

juu ya madhabahu, na juu ya matoleo yafanywayo kwa Yahweh

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : " Yahweh. : "juu ya sadaka za kuteketezwa kwa Yahweh"

naye mtu huyo atakuwa amesahewa.

Hili laweza kutamkwa kama mtindo tendaji. : "Yahweh atasamehe dhambi za mtu huyo"

Leviticus 5:14

dhambi dhidi ya vitu ambavyo ni vya Yahweh

Hii inamaanisha kwamba mtu aliyefanya dhambi kwa kutotoa kwa Yahweh kile alichomwamru Yahweh kutoa. : "Natenda dhambi kwa kushindwa kutoa kwa Yahweh kilicho cha Yahweh"

thamani yake halisi itatathminiwa kulingana na shekeli za fedha

Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji: "Naye yapasa kuamua ni shekeli ngapi huyo kondoo dume anastahili"

shekeli

Sheli ni kama gramu 11 hivi katika uzito.

shekeli za patakatifu

Labda huenda hii humaanisha kulikuwa angalau na njia mbili za kupima shekeli. Hii humaanisha namna kuhani wa patakatifu alivyopima shekeli. : ""kipimo rasimi katika hema takatifu"

patakatifu

Hili ni jina lingine la hema takatifu

ataongeza moja ya tano

ya tano - Hii inamaanisha mtu huyo alilazimika kulipa ziada ya moja ya tano ya thamani ya alichodaiwa na Yahweh.

moja ya tano

ya tano - Hii ni sehemu moja kutokana na sehemu tano zilizosawa.

Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake

Ile nomino dhahania "upatanisho" yaweza kutamkwa kama kitenzi. "kuhani atapatanisha kwa ajili yake"

naye mtu huyo atakuwa amesamehewa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "yahweh atamsamehe mtu huyo"

Leviticus 5:17

ameagiza lisitendwe

Hii yaweza kutakwa katika mtindo tendaji. : ": "amewaamuru watu wasitende

atachukua hatia yake mwenyewe

Ile hatia ya mtu imezungumziwa kana kwamba ni kitu kinachoonekana ambacho mtu hukibeba. Neno "hatia" hapa huwakilisha kwa hatia hiyo. : "naye anawajibika kwa hatia yake mwenyewe" au "Yahweh atamwadhibu yeye kwa dhambi zake"

mwenye thamani ya fedha iliyopo

Hii humaanisha kuwa mtu huyo ni lazima aamue kwa kutumia kipimo rasimi cha kwenye hema takatifu ni kiasi gani cha shekeli huyo kondoo dume anastahili.

naye atakuwa amesamehewa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Yahweh atamsamehe yeye"

na kwa hakika amekuwa na hatia mbele za Yahweh."

"Hakika Yahweh ataiangalia hatia yake"

Leviticus 6

Leviticus 6:1

kuvunja amri dhidi ya Yahweh

"aasiye mojawapo ya amri za Mungu"

kujishughulisha na uongo dhidi ya jirani yake kuhusu kitu fulani kilichowekwa amana kwake

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. : "akidanganya kwa jirani yake kuhusu kitu fulani alichomwazimisha yeye

jirani yake

"Jirani yake" humaanisha Mwisraeli yeyote, siyo yeyote aishiye karibu naye.

alichokichukua kwa dhuluma kutoka kwake

Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "bila kurudisha kitu fulani alichokiazima"

Leviticus 6:5

kwa ukamilifu

"kikamilifu" au "kabisa"

kuongeza moja ya tano

Tazama lilivyotafsiriwa katika 5:15

kumlipa anayedai

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. :"kulipa mtu anayemdai"

anayopatikana na hatia

Mtu aliyeiba yapasa kuletwa mbele ya mwamuzi na kutangazwa mwanyehatia. : "sentensi hii yaweza kutamkwa katika mtindo tendaji. "hakimu anamtangaza kuwa mwenye hatia"

inayolinga na thamani ya sasa

Tazama 5:14 uone lilivyofasiriwa

Naye kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake

Ile nomino dhahania "upatanisho" yaweza kutamkwa kama kitenzi. : "kuhani atapatanisha kwa ajili yake"

mbele ya Yahweh,

katika uwepo wa Yahweh"

naye atakuwa amesamehewa

Hii humaanisha Yahweh atamsamehe mtu huyo, siyo kuhani. Hii yaweza kutafasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Mungu atamsamehe yeye"

Leviticus 6:8

Kisha Yahweh akazungumza na Musa akisema, "Mwagize Aroni na wanawe, kusema, 'hii ndiyo sheria

Hii ina nukuu ndani ya nukuu. nukuu ya moja kwa moja yaweza kutamkwa kama nukuu taarifa yenyekutajwa. : "Kisha Yahweh akazungumza na Musa na kumwambia kumwamru Aroni na wanawe, akisema, 'Hii ndiyo sheria'"

juu ya meko ya madhabahu

"Lazima iwe juu ya madhabahu"

nao moto wa madhabahu utaendelea kuwaka.

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yapasa uufanye moto wa madhabuni uendelee kuwaka"

Leviticus 6:10

nguo zake za kitani,

Kitani ni nguo nyeupe. : "nguo zake nyeupe"

Naye atayachukua hayo majivu

"Naye atayakusanya hayo majivu"

baada ya moto kuwa umetekeza sadaka ya kuteketezwa

Moto kuteketeza kabisa sadaka umezunguzwa kana kwamba umeitafuna au kuitumia sadaka ya kutekezwa

mpaka mahali palipo safi

Mahali panapofaa kutumika kwa makusudi ya Mungu pameongelewa kana kwamba palikuwa safi kimaumbile.

Leviticus 6:12

Huo moto ulio juu ya madhabahu utaendelea kuwaka.

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Kuhani atautunza moto ulio juu ya madhabahu ili uendelee kuwaka"

kama inavyotakiwa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "juu yake kama Yahweh anavyotaka"

Leviticus 6:14

kuleta harufu ya kupendeza

Tazama sura 1:7 lilivyofasiriwa kama kirai kile kile.

sadaka ya kuwakilisha

Tazama lilivyotafsiriwa sura ya 2:1

Leviticus 6:16

ni lazima iliwe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. : "Yawapasa kuila"

Haitaokwa pamoja na hamira

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "msiioke na hamira"

matoleo... yafanywayo kwa moto

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "sadaka za kuteketeza"

Yeyote ayagusaye atakuwa mtakatifu."

Hili ni onyo limaanishalo kwamba hao walio wa uzao wa Aroni wasio wanaume haikuwapasa kuigusa hiyo sadaka. Maana kamili ya kauli hii yaweza kuwa wazi.

Leviticus 6:19

ambayo kila mwana atapakwa mafuta

hii inamaanisha kwamba watapakwa mafuta watakapokuwa makuhani. Maana ya kamili ya kauli yaweza kuwekwa wazi. Hii pia yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Anapompaka mafuta kila mwana, akiwaweka wakfu kuwa makuhani"

sehemu ya kumi ya efa

Efa moja ni sawasawa na lita 22. moja ya kumi ya efa ni kama lita 2 hivi.

sehemu ya kumi

Hii ni sehemu ya kumi sehemu zilizosawa.

Leviticus 6:21

Nayo Itatengenezwa

hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Nawe utaitengeneza"

katika kikaango

Tazama sura ya 2:4 uone lilivyofasiriwa.

Itakapokuwa imelowekwa

"Unga unapokuwa umeloana kabisa kwa mafuta"

utaileta ndani

Hapa "Nawe" humrejelea mtu anayetoa sadaka.

ili kuleta harufu ya kupendeza kwa Yahweh

Tazama maelezo katika sura ya 1:7 kwa ufafanuzi.

Kama ilivyoamriwa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Kama vile ambayo Yahweh amekuamru"

yote itateketezwa

Hii yaweza kutakwa katika mtindo tendaji. : "yapasa aiteketeze yote"

itateketezwa yote kabisa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Yapasa aiteketeze yote kabisa"

Haitaliwa kamwe

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Hakuna apaswaye kuila"

Leviticus 6:24

Yahweh akazungumza tena na Musa, akisema, "Sema na Aroni na wanawe uwaambie kwamba, 'Hii ndiyo sheria

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Nukuu ya moja kwa moja yaweza kutamkwa kama nukuu taarifa yenyekutajwa. : "Yahweh alizungumza na Musa na akamwambia kuzungumza na Aroni na wanawe, akimwambia, 'Hii ndiyo sheria'"

Sema na Aroni na wanawe

Yahweh anazungumza na Aroni na wanawe, lakini kanuni hizi zinatekelezeka kwa makuhani. Maana kamili ya maelezo haya yaweza kufanywa wazi.

Sadaka ya dhambi lazima ichinjwe... mbele za Yahweh

Yaweza kuwekwa wazi kwamba hii hurejelea upande wa kaskazini wa madhabahu. Tazama 1:10

inapochinjwa sadaka ya kuteketezwa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji:. : "Yakupasa kuichinjwa sadaka"

Sadaka ya dhambi lazima ichinjwe

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "mahali unapomchinjia mnyama wa sadaka ya kuteketezwa"

mbele za Yahweh

"kwa Yahweh"

Nayo yapasa kuliwa

Hii yaweza kutmkwa katika mtindo wa utendaji. : "Yampasa kuila"

Leviticus 6:27

Chochot kigusacho nyama yake kitakuwa kitakatifu

Hili ni onyo linalomaanisha kwamba zaidi ya makuhani hakuna impasaye kugusa nyama ya sadaka ya dhambi. Maana kamili ya maelezo haya yaweza kuweka wazi.

kama damu yake inanyunyizwa juu

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. : "iwapo damu yake inanyunyizwa juu"

chungu ambamo inachemshiwa lazima kivunjwe

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "yakupasa kukivunja chungu ambacho ndani yake uliichemshia"

kama imechemshwa ndani ya chombo cha shaba, lazima kisuguliwe na kusafishwa kwa maji

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "kama ulichemsha nyama kwenye kwenye sufuria ya shaba, hivyo itakupasa kuisugua sufuria na kuisuuza kwa maji safi"

Leviticus 6:29

sadaka ya dhambi...haitaliwa

Hii yaweza kutamkwa ktika mtindo wa utendaji. "Hakuna hata mmoja atakayeila sadaka ya dhambi"

ambayo damu yake inaletwa kwenye hema la kukutania

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. ; Amabayo kutoka kwayo kuhanai anatoa damu ya kuleta kwenye hema la kukutania"

Ni lazima iteketezwe.

Hii yaweza kutamkwa ktika mtindo wa utendaji. : "lazima Kuhani ataiteketeza"

Leviticus 7

Leviticus 7:1

Taarifa kwa Ujumla:

Yahweh anaendelea kumwambia Munsa kile anachopaswa kumwambia Aroni na wanawe.

mahali panapostali kuchinjwa

Panaweza kuwekwa wazi kwamba hapa panamaanisha Mahali ambapo wanyama watolewao kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa huchinjwa. Tazama 1:10

Mafuta yote yaliyomo ndani yake yatatolewa:

Hii yaweza kufasiriwa katika mtido wa utendaji. : "Yule kuhani atayatoa mafuta yote yaliyomo ndani yake"

sehamu za ndani

Hili ni tumbo pamoja na Matumbo

Ini...figo

maneno haya yamefasiriwa katika mtindo ule ule uliotumika kwenye sura ya 3:3

karibu na kiuno

Hii ni sehemu ya mwili kwenye pande za uti wa mgonngo kati ya mbavu na mifupa ya nyonga. Tazama 3:3

hii yote lazima iondolewe

Hili linaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : Huyo Kuhani aiondoa hii yote.

Leviticus 7:5

viwe dhabihu iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "viwe sadaka ya kuteketezwa"

lazima iliwe

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Ni lazima waile"

Leviticus 7:7

Ni sheria ileile hutumika kwa zote mbili

"Sheria ni ileile kwa zote mbili"

ya kuhani azitumiaye kufanya upatanisho.

Ile nomino dhahania "Upatanisho" yaweza kutamkwa kama kitenzi. : "kwa kuhani aitoaye dhabihu ili kupatanisha kwa aji;li ya dhambi za mtu fulani"

ngozi

Vazi au ngozo ya mnyama

Leviticus 7:9

inayookwa mekoni... ipikwayo kaangoni

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Ile ambayo mtufulani anaioka mekoni... ile ambayo mtu fulani huipika mekoni"

Meko

Tazama maelezo katika sura 2:3

Kaango

Tazama maelezo katika 2:6 ili uone neno "kaango" lilivyotafsiriwa

Sufuria

Tazama sura ya 2:4 uone neno "sufuria" lilivyofasiriwa

Leviticus 7:11

mikate isiyotiwa hamira, bali iliyochanganywa na mafuta ya zeituni

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ya mikate aliyoifanya pasipo kutia hamira bali kwa kuchanganya na mafuta.

vipande vya mkate...iliyochanganywa na mafuta ya zeituni

"Vipande vya mkate" hapa humaanisha mkate mnene

kaki zisizotiwa hamira, lakini ziwe zimefanywa kwa mafuta ya zeituni yaliyopakwa juu yake

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji: : ya mikate miembamba aliyoifanya bila hamira bali kwa kuipaka mafuta"

kaki...zilizopakwa mafuta

"Kaki" hapa humaanisha mkate mwembamba.

mikate iliyofanywa kwa unga laini uliochanganywa vema na mafuta

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ya mikate aliyoitengeneza kwa unga laini uliochanganywa na mafuta"

mikate iliyofanywa kwa unga laini

"Mikate'" hapa humaanisha mkate mnene. Hufanana na aina ya ule mkate wa kwanza isipokuwa wenyewe unafanywa kwa unga uliolaini zaidi

Leviticus 7:13

vipande vya mikate iliyotiwa hamira

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji: : : "vipande vya mkate alioufanya kwa kutia hamira"

vipande vya mkate

Hii humaanisha mkate mnene.

Leviticus 7:15

Mtu anayeleta

"Mtu anayetoa"

kwa kusudi la kutoa shukrani

Ile nomino dhahania "shukurani" yaweza kutamkwa kama kitenzi. : "kwa kusudi la kumshukuru Yahweh"

lazima nyama italiwa...kinaweza kuliwa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ni lazima aile hiyo nyama...anaweza kuila"

Leviticus 7:17

katika siku ya tatu

ya tatu hii ni namba ya kawaida kwa tatu. : "baada ya siku mbili"

lazima ichomwe moto

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. " : "mtu anayepaswa uiteketeza"

Iwapo kipande chochote cha nyama hiyo ya dhabihu kinachobaki kinaliwa katika siku ya tatu

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "iwapo mtu yeyote anakula nyama yake ya sadaka

hakitakubalika

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Yahweh hataikubali"

wala hakitatolewa kwa aliyeitoa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "wala Yahweh hataiheshimu dhabihu ambayo huyo mtu aliitoa"

atabeba hatia ya dhambi mwenyewe yake

Mtu anayewajibika kwa dhambi aliyoitenda anazungumziwa kana kwamba anapaswa kubeba kimaumbile hiyo hatia.

Leviticus 7:19

9Nyama yoyote igusayo kitu kilicho najisi haitaliwa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Hakuna awezaye kula nyama inayogusa kitu fulani kilichonajisi"

kitu kilicho najisi

Kitu fulani ambacho Yahweh amekitamka kuwa hakifai kukigusa au kukila kinasungumziwa kana kwamba kilikuwa najisi kimaumbile.

Ni lazima iteketezwe kwa moto

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yapasa uiteketeze kwa moto"

yeyote aliye safi

Mtu mwenye kukubalika kwa kusudi la Mungu anazungumziwa kana kwamba ni mtu aliyekuwa safi kimaumbile.

mtu yeyote aliyenajisi

Mtu asiyekukubalika kwa kusudi la Mungu anazungumziwa kana kwamba ni mtu aliyekuwa mchafu kimaumbile.

yapasa mtu huyu akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake.

Mtu anayetengwa kutoka kwa jamii yake anazungumziwa kana kwamba amkwisha kukatwa kutoka kwa watu wake, kama vile mtu akatavyo kipande cha nguo au tawi kutoka kwenye mti. : "mtu huyo hawezi kuishi miongoni mwa watu wake" au "yapasa umtenge mtu huyo kutoka kwa watu wake"

Leviticus 7:21

kitu chochote kilichonajisi

Kitu fulani ambacho Yahweh amekitaja kuwa hakifai kugusa au kula kinazungumziwa kana kwamba kilikuwa si safi kimaumbile.

iwe ni unajisi wa binadamu, au wa mnyama aliyenajisi,

"Mtu" hapa mumaanisha wanadamu kwa ujumla. : "ikiwa wa mtu au wa mnyama

au wa kitu fulani kilichonajisi na chenye kuchukiza

au wa unajisi fulani wa kitu ambacho humchukiza Yahweh

lazima mtu huyo akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake.

Tazama maelezo katia sura ya 7:19. Hii pia yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji.

Leviticus 7:22

Kisha Yahweh akazungumza na Musa, akisema, "Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, 'hamruhusiwi kula mafuta

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Nukuu ya moja kwa moja yaweza kutamkwa kama nukuu taarifa yenyekutajwa. "Kisha Yahweh na akamwambia Musa kumbia kuwaambia watu wa Israeli kwamba: "Hamtakula mafuta"

afaye peke yake bila ya kuwa dhabihu

"aliyekufa peke yake lakini hakuwa dhabihu"

mafuta ya mnyama yeyote aliyeraruliwa na wanyama pori

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "mafuta ya mnyama yule ambaye mnyamapori alimuua"

Leviticus 7:25

dhabihu iliyofanywa...kwa moto

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Sadaka ya kutekeza"

mtu huyo lazima atakatiliwa mbali kutoka kwa watu wake

Tazama katika sura ya 7:19

Hamtakula damu

"Hamtatumia damu"

katika mojawapo ya nyumba zenu

"katika masikani yenu" au "popote mwishipo"

Leviticus 7:28

Kwa hiyo Yahweh akazungumza na Musa na akasema, "Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, 'Yeye atoaye

Hii ina nukuu ndani ya nukuu. Nukuu ya moja kwa moja yaweza kutamkwa kama nukuu taarifa yenyekutajwa. : Kisha Yahweh akazungumza na Musa na akamwambia awaambie watu wa Israeli kwamba: 'Yeye atoaye"

Mikono yake mwenyewe lazima iilete hiyo sadaka ifanywayo kwa Yahweh kwa moto

Kile kirai "ifanywayo kwa moto" yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Yeye mwenyewe analazimika kuileta sadaka anayopanga kuiteketeza kama dhabihu kwa Yahweh"

Mikono yake mwenyewe

"Mikono" humwakilisha mtu mzima. : "yeye mwenyewe anapaswa kuileta"

kidari

Sehemu ya mbele ya mwili wa mnyama iliyoko chini ya shingo

ili kwamba kidari kiweze kutikiswa kuwa sadaka ya kutikiswa mbele za Yahweh.

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ili kwamba kuhani aweze kuiwasilisha kwa Yahweh kama sadaka ya kutikiswa"

kiweze kutikiswa kuwa sadaka ya kutikiswa mbele za Yahweh.

Kuiinua juu sadaka ni mfano wa ishara unaoonyesha kwamba mtu anaiweka wakfu dhabihu kwa Yahweh.

Leviticus 7:31

Paja

Sehemu ya juu ya mguu juu ya goti

kama sadaka iliyotokana

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "nawe uitoe kama sadaka"

Leviticus 7:33

Kwa kuwa nimetwaa

"Nime..." hapa humrejelea Yahweh.

uwe mchango

hiyo ninaitoa kama sadaka"

Leviticus 7:35

sadaka zilizofanywa kwa Yahweh kwa moto

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Sandaka za kuteketezwa kwa ajili ya Yahweh"

ambao Yahweh aliamru waweze kupewa kutoka kwa watu wa Israel

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "aliyowaamru Yahweh watu wa Israeli kuitoa kwao"

hiyo aliyowatia mafuta ya upako wawe makuhani

ambayo Musa aliwapaka mafuta makuhani".

katika vizazi vyote

Hii yaweza kufasiriwa kama katia sura ya 3:15

Leviticus 7:37

Maelezo Unganishi

Huu ni mwisho wa hotuba iliyoanzia katika 7:28

Leviticus 8

Leviticus 8:1

Taarifa kwa ujumla

Katia sura ya 8 Musa anawaweka wakfu Aroni na wanawe wawe makuhani kulingana na aagizo ya Yahweh ambayo aliyaamru katika kitabu cha Kutoka

mavazi

"Mavazi ya kikuhani" au "nguo walizavaa makuhani"

Leviticus 8:4

Haya ndiyo Yahweh amegiza yatendwe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Yahweh alituamru sisi kutenda"

Leviticus 8:6

na kuwaosha kwa maji

Hili ni tendo la kiishara. Ni usafishaji wa kiibada ambao huwandaa wao kuwa makuhani.

kanzu... ukumbuu...joho...kizibao...mshipi uliosokotwa kwa ustadi

mshipi uliosokotwa kwa ustadi - Haya ni mavazi ambayo Yahweh aliwaamru watu kutengeneza kwa ajili ya makuhani.

ukumbuu`

kipande cha nguo kirefu ambacho kinafungwa kuzunguka kiuno au kifua.

kukikaza mwilini mwake

"alikifunga kumzunguka"

Leviticus 8:8

akaweka kifuko kifuani mwa Aroni

"Musa aliweka kifuko juu ys |Aroni"

kifuko kifuani..kiremba...bamba la dhahabu... taji takatifu

Haya yote ni mavazi maalum ambayo Yahweh aliwaamru watu kutengeneza kwa ajili ya makuhani.

Urimu na Thumimu

Hivi havikujulikana wazi vilikuwa ni vitu gani. Vilikuwa vitu ambavyo kwa kuhani alivitumia kwa namna fulani kupambanua mapenzi ya Mungu.

kiremba

kifuniko cha kicho cha mtu ambapo kilikuwa ni kitambaa cha nguo kirefu kilichofungwa kukizunguka kichwa

bamba la dhahabu; liwe taji takatifu

Virai hivi viwili hurejelea kitu kile kilekile. Lilikuwa ni mamba la dhahabu tupu lililoambatanishwa na kiremba.

Leviticus 8:10

vyombo vyake vyote

Hivi vyote ni vyungu, masufuria, makoleo, na nyuma vilivyotukaka kwenye madhabahu.

sinia la kunawia

Hili ni besenni la shaba liliowekwa kati ya madhabahu na hema.

kitako chake

Hiki ni kinara cha shaba ambacho juu yake sinia la kunawia liliwekwa.

Leviticus 8:12

Akamimina

"Musa alimimina"

ukumbuu

Tazama lilivyofasiriwa katika sura ya 8:6

Leviticus 8:14

wakaweka mikono yao juu ya kichwa

Tazama jinsi lilivyofasiriwa katika sura ya 1:3

mpembe za madhabahu

Tazama jinsi lilivyofasiriwa katika sura ya 4:6

kuitenga kwa Mungu

"tenga madhabahu kwa ajili ya Mungu"

kufaa kwa kufanyia upatanisho.

"Upatanisho" hapa humaanisha kuifanya madhabahu ifae katika kumtumikia Mungu. : "ili kuifanya mahali pa kufaa kwa ajili ya kuteketezea dhabihui ya dhambi"

Leviticus 8:16

sehemu za ndani

Tazama lilivyofasiriwa katika sura ya 1:7

ini...figo

Tazama lilivyofasiriwa katika sura ya 3:3

ngozi

Hili ni vazi au nyama ya juu yenye manyoya ya mwili wa mnyama wa kundini

Leviticus 8:18

wakaweka mikono yao juu ya kichwa

Tazama lilivyofasiriwa katika sura ya 1:3

Leviticus 8:20

Naye akamkatakata kondoo

"Musa akamkata kondoo"

ilitoa harufu ya kupendeza

Tazama lilivyofasiriwa katika sura ya 1:7

sadaka iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Sadaka aliyoiteketeza kwa Yahweh"

Leviticus 8:22

kondoo wa kuwekwa wakfu

Neno "kuweka wakfu" ni nomino dhahania. : "kondoo kwa ajili ya kuwatenga Aroni na wanawe kwa ajili ya huduma ya Mungu"

wakaweka mikono yao juu ya kichwa

Tazama lilivyofasiriwa katika sura ya 1:3

naye akaweka sehemu ya damu ya kondoo

Inaonesha kwamba Musa aliikinga damu kwenye bakuli wakati ilipochuruzika kutoka kwa mnyama. Maana yake yaweza kuwekwa wazi

Leviticus 8:25

sehemu za ndani

Tazama lilivyofasiriwa katika sura ya 1:7

ini...figo

Limefasiriwa kama ilivyofanyika katika sura ya 3:3

paja la kulia

Tazama lilivyofasiriwa katika sura ya 7:31.

kikapu cha mikate isiyo na hamira ambayoo ilikuwa mbele za Yahweh

Hii haimaanishi mahali pa kikapu cha mikate. humaanisha kwamba huu ni mkate ambao Musa amishauweka wakfu kwa Yahweh.

weka mikoni mwa Aroni na katika mikono ya wanawe

"Mikono" hapa huwakilisha nafsi nzima. : "aliitoa yote kwa Aroni na wanawe"

kuvitikisa mbele za Yahweh kuwa sadaka ya kutikiswa

Inaashiria kwamba Aroni na wanawe waliiwasilisha sadaka. Maana kamili ya tamko hili yaweza kufanywa ya kueleweka. :"Walivitikisa mbele za Yahweh kuwa sadaka ya kutikiswa"

kuitikisa

Hili ni tendo la kiishara linaloweka wakfu sadaka kwa Yahweh.

Leviticus 8:28

Musa akaichukua

sherehe rasmi inayomfanya mtu kuwa kuhani

kutoka mikononi mwao

"Mikono" hapa huwakilisha nafsi nzima. : "kutoka kwa Aroni na wanawe"

Zilikuwa ni sadaka ya kuwekwa wakfu

"Zilikuwa sadaka za kuwatenga Aroni na wanawe kwa ajili ya huduma kwa Yahweh"

sadaka iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Sadaka ya kuteketezwa kwa Yahweh kwa moto

ilitoa harufu ya kupendeza

Tazama lilivyofasiriwa katika sura ya 1:7

kidari

Sehemu ya mbele ya mwili wa mnyama chini ya shingo

kuwekewa mikono

Sherehe rasmi inayomfanya mtu kuwa kuhani

Leviticus 8:30

Musa

Musa alikuwa nabii na kiongozi wa watu wa Musa alipokuwa mtoto, wasazi wake Musa walimweka kwennye kikapu kwenye mianzi ya mto Nile ili kumficha kutoka kwa Pharao wa Misri. Miriamu, dada yake Musa alimwangalia huko. Maisha ya Musa yalilindwa tu pale binti Farao alipomwona na kumpeleka ikulu kumlea kama mwanawe.

Mungu allimchagua Musa kuwaokoa Waisraeli kutoka utumwani Misri na kuwaongoza mpaka nchi ya ahadi.

Baada kuundoka kwa Waisraeli huko Misri, na wakiwa wanarunguka jangwani, Mungu alimpa Musa mbao mbili za mawe zilizoandikwa Amri za Mungu juu yake.

Karibu na mwisho wa uhai wake, Musa aliitazama tu nchi ya ahadi, lakini hakuingia kuishi humo kwa sababu hakumtii Mungu.

Paka mafuta, mpakwa mafuta

Neno "paka mafuta" humaanisha kusugua au mimina mafuta juu ya mtu au chombo, Wakati mwingine mafuta yalichanganywa na viungo, vikiyapa harufu yenye manukato. Neno pia limetumika kitamathari kumaanisha Roho Mtakatifu kumchaguwa na kumwezesha tu.

Katika Agano la Kale, makuhani, wafalme na manabii walipakwa mafuta ili kutenga kwa huduma maalum kwa Mungu.

Vyombo kama vile madhababhuau hema, vilipakwa mafuta kuonyesha kwamba vilikuwa vitumike kumwabudia na kumtukuza Mungu.

Katika Agano Jipya, wagonjwa walipakwa mafuta kwa uponyaji wao.

Agano Jipya hutaarifu mara mbili amabapo Yesu alipopakwa yenye manukato na wanawake, kama tendo la ibada. Wakati mmoja Yesu alisifia kwamba kwa kufanya hivi mwanamke huyo alikuwa akiandaa maziko Yake ya baadaye.

Yesu alipokufa, rafiki zake waliuandaa mwili wake kwa maziko kwa kuupaka mafuta na uvumba.

Vyeo "Mesiya" (Kiebrania) na "Kristo" (Kiyunani) humaanisha "Mpakwa mafuta"

MAPENDEKEZO YA UFASIRI

Kutegemeana na muktadha, neno "paka mafuta" laweza kufasiriwa kama "mimina mafuta juu ya" au "weka mafuta juu ya" au "weka wakfu kwa kumminia mafuta yaliyotiwa manukato."

"Kupakwa mafuta" laweza kufasiriwa kama "wekwa wakfu kwa kupakwa mafuta." au "teuliwa" au "wekwa wakfu."

Katika baadhi ya mazingira neno "paka mafutaa" linaweza kufasiriwa kama "teuwa."

Kirai kama "kuhani mpakwa mafuta," laweza kufasiriwa kama "kuhani aliyewekwa wakfu kwa mafuta" au kuhani aliyetengwa kwa miminiwa mafuta juu yake."

damu

Neno "damu" humaanisha kimiminika chekundu ambacho hutoka katika ngozi ya mtu kunapoukuwa na jeraha au kovu. Damu hutoa virutubisho viletavyo uhai katika mwili mzima wa mtu.

Damu huashiria uhai na inapomwagwa, huashiria kupoteza maisha au kifo.

Watu walipofanya dhabihu kwa Mungu, waliua mnyama na walimimina damu juu ya madhabahu. Hii iliifananisha dhabihu ya uhai wa damu ya mnyama

Mafuta

Mafuta ni kimiminika kizito, safi kilichotokana na mimea au matunda fulani. Kwa kawaida katika nyakati za Biblia yalitokana na mizeituni.

Mafuta ya zeituni yalitumika kwa kupikia, kupaka, dhabihu, taa, na dawa.

katika nyakati za kale, mafuta ya zeituni yalikuwa na gharama kubwa na umiliki wa mafuta ulihesabika kama kipimo cha utajiri.

Madhabahu

Madhabahu ni muundo ulionuliwa juu ambao juu yake Waisrali waliteketeza wanyama na nafaka kama sadaka kwa Mungu.

Nyakati za Biblia, mara kwa mara watu walitengeneza madhabahu rahisi kwa kuumba rundo la undongo uliofungashwa au kwa kupanga mawe makubwa kwa ungalifu ili kufanya rundo imara.

Baadhi ya madhabahu zilitengenezwa kwa kuunda makasha maalum kwa mbao zilizofunikwa kwa metali kama vile dhahabu, shaba nyeupe au shaba nyekundu.

Baadhi ya makundi mengine ya watu jirani na Israeli pia walijenga madhabahu ili kutoa dhabihu kwa miungu yao.

tenga

Neno "tenga" humaanisha kutengwa na jambo fulani ili kutimiza kusudi fulani.

Waisraeli walitengwa kwa huduma ya Mungu.

Roho Mtakatifu aliwaamru Wakristo wa Antiokia kuwatenga Paulo na Barnaba kwa kazi ya Mungu aliyowataka wao waifanye.

Mwamini "aliyetengwa" kwa kazi ya Mungu "amewekwa wakfu" kutimiza mapenzi ya Mungu.

Moja ya maana ya "mtakatifu" ni kutekwa kuwa wa Mungu na kuwa umetengwa kutoka katika njia za dhambi za ulimwengu.

Ule msamiati "takasa" humaanisha kumtenga mtu kwa huduma ya Mungu.

MAPENDEKEZO YA UFASIRI Njia za kufasiri "kutenga" zaweza kujumuisha, "kuchagua mahususi" au kutenga kutoka miongoni mwenu" au "kuweka kando ili kufanya kazi maalum."

"Kutengwa" kwaweza kufasiriwa "kuwekwa kando

Vaa, vikwa

Neno "kuvikwa na" linapotumika kitamathli kwenye Biblia, humaanisha kuruzukiwa au kuandaliwa kwa kitu fulani. "Kujivika" mwanyewe na kitu fulani humaanisha kutafuta kuwa na tabia yenye sifa fulani.

MAPENDEKEZO YA UFASIRI Kama inawezekana, ni vema kuitunza tamathali ya usemi, "jivike na." Njia nyingine ya kufasiri hili ni yaweza kuwa "vaa" kama hii ingemaanisha kuvaa nguo.

Kama hii haileti maana sahihi, njia nyingine ya kuifasiri tamathali "kuvikwa na" yaweza kuwa "kuonyesha" au "kudhihirisha" au kujazwa na" au kuwa na sifa ya."

Neno "jivike na" laweza pia kufsiriwa kama "jifunike na" au "enenda katika njia ambayo huonyesha."

mwana, mwana wa

Neno "mwana" hurejelea mvulana au katika uhusiano kwa wazazi. Laweza pia kumaanisha ama mzao mwanaume wa mtu fulani au kwa mwana aliyeasiliwa.

"Mwana," mara kwa mara limetumika kimafumbo katika Biblia kumaanisha mzao yeyote wa kiume, kama vile mjukuu au kitukuu.

Neno "mwana" pia linaweza kutumika kama muundo wa kistaraabu wa kumwita mvalana au mtu aliye kijana.

Wakati mwingine "wana wa Mungu" limetumika kwenye kumaanisha waaminio katika Kristo.

Mungu anaiita Israeli "mwanawe mzaliwa wa kwanza." Hii hurejelea uchaguzia wa Mungu wa taifa la Israeli kuwa watu maalum wa Mungu. Ni kwa kupitia kwao kwamba ujumbe wa ukombozi na wokovu ulikuja, ukiwa na matokeo yake kwamba watu wengi wamefanyika watoto wa kiroho.

Kirai "mwana wa" mara kwa mara limekuwa na maana ya kimafumbo, "kikiwa na sifa bainishi za." Mifono ya hiki hujumuisha wana wa nuru," "wana wa amani," na "wana wa ngurumo."

Kirai "mwana wa" pia kimetumika kuzungumzia ni nani aliye baba wa mtu. Kirai hiki hutumika kuelezea vizazi na maeneo mengine mengi.

Kwa kutumia "mwana wa" kwa kutoa jina la baba mara mara husaidia kutofautisha watu wenye majina yenye kufanana. Kwa mfano, "Azaria, mwana wa Sadoki" na Azaria, mwana wa katika 1 Wafalme 4, na "Azaria, mwana wa Amazia" katika 2 Wafalme 15 ni watu watatu waliotofauti.

MAPENDEKEZO YA UFASIRI Kwenye muktadha wa kukiri kwamba kitu fulani ni kweli, "kiri" laweza kufasiriwa kama "kubali" au "tangaza" au "ungama" kuwa ni kweli au "amini."

Linapomaanisha kumtambua mtu, neneo hili laweza kufasiriwa kama "pokea" au "tambua" uthamni wa" au ambia wengine kwamba

Leviticus 8:31

kikapu cha kuwekwa wakfu

Hii humaanisha kikapu kilicho na matoleo yatumikayo wakati wa kuwaweka wakfu Aroni na wanawe. : "kile kikapu"

kama nilivyoamru, kusema, 'Aroni na wanawe wataila

Hii ina nukuu ndani ya nukuu. Nukuu ya moja kwa moja yaweza kutamkwa kama nukuu isiyo ya moja kwa moja. " kama nilivyokuagiza kufanya"

hata zitakapotimia siku za kuwekwa mikono kwenu

Hii yaweza kufasiriwa katiika mtindo wa utendaji. : "mpaka mkamilishe siku zenu za kuwekewa mikono.

kuwekwa mikono

Tazama lilivyofasiriwa katika sura ya 8:28

Leviticus 8:34

Kitendeke

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "sisi tutende"

Kufanya upatanisho kwa ajili yenu

Ile Nomino dhahania "upatanisho" yaweza kutamkwa kama kitenzi. : " Kupatanisha kwa ajili ya dhaambi zenu"

hivi ndivyo nimeamriwa

Hii yaweza kufasiriwakatika mtindo wa utendaji. "hivi ndivyo ameniamru"

Leviticus 9

Leviticus 9:1

siku ya nane

Neno "ya nane" ni namba ya kawaida kwa nane.

Mbele za Yahweh

"kwa Yahweh" au "katika uwepo wa Yahweh"

Leviticus 9:3

Maelzo jumla:

Musa anaendelea kumwambia Aroni'

Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, 'Twaeni beberu...atajidhihirisha kwenu

Musa anaendelea kumwambia Aroni. Sentensi hii ina nukuu ndani ya nukuu. Nukuu ya moja kwa moja kwa moja yaweza kutamkwa kama nukuu taarifa iliyotwa. : "na waambie watu Israeli watwae beberu...atajidhihirisha kwa watu wote"

wa umri wa mwaka moja

"mwenye umri wa miezi kumi na miwili"

ilikuwatoa mbele za Yahweh

"kutoa kwa Yahweh"

Leviticus 9:6

amewaamru nyinyi mfanye

"Nyinyi" hapa humaanisha watu wa Israeli.

ili kwamba utukufu wake uweze kuonekana kwenu

"Utukufu" hapa huwakilisha uwepo wa Yahweh. : ""ili kwamba aweze kuonyesha utukufu wa uwepo wake"

kufanya upatanisho kwa ajili yako mwenyewe.. na kwa ajili ya watu ili kufanya upatanisho kwa ajili yao

Hizi ni dhabihu mbili tofauti. Dhabihu ya kwanza ni kupatanisha kwa ajili ya dhambi za kuhani mkuu. Kuhani mkuu anapotenda dhambi, hiyo dhambi huwafanya watu wawe na hatia. (Tazama 4:1) Dhabihu ya pili ni kupatanisha dhambi za watu wanazotenda wenyewe.

Leviticus 9:8

wana wa Aroni wakamletea hiyo damu

Hii inaonyesha kwamba waliikinga damu kwenye bakuli wakati damu ilipokuwa ikichuruzika kutoka kwa mnyama. Maana kamili ya tamko hili yaweza kufanywa wazi wazi

pembe za madhabahu

Tamza maelezo ya sura ya 4:6

chini ya kitako cha madhabahu

"chini ya madhabahu"

Leviticus 9:10

aliyateketeza

"Aroni aliiteketeza"

figo...ini

Tazama maelezo ya sura ya 3:3

ngozi

Tazama maelezo ya sura ya 7:7

Leviticus 9:12

wanawe wakampa hiyo damu

Tazama maelezo ya sura ya 9:8

sehamu za ndani

Tazama maelezo ya sura ya 1:7

Leviticus 9:15

mbuzi wa kwanza

Neno "wa kwanza" ni namba ya mpango kwa ajili ya namba moja. : "mbuzi kwa ajili ya sadaka yake mwenyewe.

pamoja na sadaka ya asubuhi ya kuteketezwa

Hii humaanisha dhabihu ya kwanza ya kila siku. kuhani angieitoa dhabihu hii ya kuteketezwa asuhubi kabla ya dhabihu nyingine yot yote. Maana kamili yaweza kufanywa wazi.

Leviticus 9:18

Akamchinja

"Aroni alichinja"

wana wa Aronni wakampa damu

Inamaanisha kwamba damu ilikuwa kwenye bakuli. Maana kamili yaweza kufanywa wazi.

Sehemu za ndani

Tazama maelezo ya sura ya 1:7

figo...ini

Tazama maelezo ya sura ya 3:3

Leviticus 9:20

Wakazichukua hizi sehemu

"wana wa Aroni walizichukua hizo sehemu"

wakaziweka hizi

Neno "hizi" hurejelea mafuta na sehemu zilizoorodheshwa hapo awali.

vidari

Tazama amaelezo ya sura ya 7:28

paja la kulia

Tazama amaelezo ya suru ya 7:31

mbele za Yahweh

"kwa Yahweh"

Leviticus 9:22

kisha akashuka chini

Kirai "akashuka chini" kimetumika kwa sababu mahali pa madhabahu palikuwa juu zaidi ya mahali watu walipokuwa wanasimama.

utukufu wa Yahweh ukaonekana kwa watu wote

"Utukufu" hapa huwakilisha uwepo wa Yahweh. : "Yahweh akawaonyesha watu wote utukufu wa uwepo wake"

Moto ukashuka kutoka kwa Yahweh na ukairamba

"Yahweh alituma moto ulioiramba"

ukairamba sadaka ya kuteketezwa

Moto ukiitekeza kabisa sadaka umezungumziwa kana kwamba moto uiitafuna au kuitumia sadaka ya kutekezwa.

wakala wakiinamisha nyuso zao chini

"walilala wakaelekeza nyuso zao ardhini." Hii ni ishara ya heshima na adhama.

Leviticus 10

Leviticus 10:1

Nadabu na Abihu

Haya ni majina ya wana wa Aroni

kifukizo

chombo cha metali chenye kina kifupi ambacho makuhani walikitumia kubebea makaa ya moto au uvumba

wakakaweka moto ndani yake

"akaweka makaa yaliyowaka moto ndani yake"

wakatoa moto usiokuabalika mbele za Yahweh, moto ambao hakuwaamru wao kuutoa

"Lakini Yahweh hakuikubali sadaka yao kwa sababu haikuendana na kile ambacho aliwaamru kukitoa"

moto usiokuabalika mbele za Yahweh

"moto usiokubalika kwa Yahweh"

Kwa hiyo moto ukashuka chini mbele za Yahweh

"Kwa hiyo Yahweh akatuma moto"

ukashuka chini mbele za Yahweh

"ulikuja kutoka kwa Yahweh"

na kuwala

Moto ukiwaunguza kabisa watu unazungumziwa kana kwamba uliwala au uliwatumia kabisa.

nao wakafa mbele za Yahweh

"walikufa katika uwepo wa Yahweh"

Leviticus 10:3

"Hiki ndicho Yahweh alichokuwa akikiongelea aliposema, 'Nitaufunua utakatifu wangu... mbele za watu wote'"

Hii ina nukuu ndani ya nukuu. Nukuu halisi yaweza kutamkwa kama nukuu taarifa iliyotajwa. : "Hiki ndicho Yahweh alichokuwa akiongelea alliposema kwamba angefunua takatifu wake...wamkaribiao yeye, na ya kwamba yeye atatukuzwa...watu

Nitaufunua utakatifu wangu kwa wale wanikaribiao

Kile kirai "wale wanikaribiao" humaanisha makuhani wamtumikiao Yahweh. "Nitawaonyesha wale ambao hukaribia kunitumikia kwamba Mimi ni mtakatifu" au "Wale wanaokuja karibu ili kunitumikia lazima wanitendee kama mtakatifu.

Nami nitatukuzwa mbele za watu wote

Sehemu hii ya pili ya tamko la Yahweh bado linamhusu kuhani, ambaye ni mmoja wa wanaomkaribia Yahweh. "Laazima wanitukuze mbele za watu wote" au "Lazima waniheshimu katika uwepo wa watu wote"

Mishaeli...Elzafani...Uzieli

Haya ni majina ya watu

ndugu zenu

Hii haimanishi kwamba walikuwa ndugu halisi. "Ndugu" hapa humaanisha jamaa au binamu.

Leviticus 10:5

Hivyo wakakaribia

"Kwa hiyo Mishaeli na Elzafani wakakaribia"

kuwachukua wangali wamevaa kanzu zao za kikuhani

Waliibeba miili ya Nadabu na Abihu, ambayo ilikuwa ingali kwenye kanzu za kikuhani

Eliezari...Ithamari

Haya ni majina ya wana wa Aroni.

Msiache wazi nywele za vichwa vyenu, wala msirarue nguo zenu,

Yahweh anawaambia Aroni na wanawe wasionyeshe ishara yoyote ya nje ya huzuni au kuomboleza.

ili kwamba msije mkafa

"ili kwamba msife"

asilikasirikie kusanyiko zima

"Kusanyiko" hapa humaanisha kutaniko zima la Israeli, siyo kikundi cha viongozi tu. : "asiwakasirikie watu wote wa Israeli"

nyumba yote ya Israeli

"Nyumba" hapa huwakilisha watu wa Israeli. "watu wote wa Israeli"

kwa ajili ya hao ambao Yahweh amewaangamiza kwa moto

"kwa ajili ya wale ambao Yahweh aliwaua kwa moto wake"

Leviticus 10:8

Hii itakuwa

"Hii" hapa hurejea nyuma kwenye amri kwa ajili ya makuhani ya kutokunywa mvinyo na kinywaji kikali waingiapo kwenye hema la kukutania.

amri ya kudumu katika vizazi vyote vya watu wenu

Tazama maelezo ya sura ya 3:15.

ili kupaambanua

Unaweza kuanza sentensi mpya hapa. "Yawapasa mfanye hivyo ili kwamba muweze kutofautisha"

kati ya mambo matakatifu na mambo ya kawaida

Yale majina vumishi "mataktifu" na "ya kawaida" yaweza kutamkwa kama vivumishi. : "Kati ya kilicho kitakatifu na "cha kawaida" au "kati ya kilichowekwa wakufu kwa Mungu na kilicho cha kawaida

kati ya kilichonajisi na kilichosafi

Yale majina vumishi "kilichonajisi|" na "kisichosafi" yaweza kutamkwa kama vivumishi. : "Kati ya kinajisi na kisafi" au "kati ya kile Mungu ambacho Mungu hatakikubali na kile ambacho atakikubali"

Kilichonajisi

Mtu au kitu ambacho Yahweh amekitamka kuwa hakifai kuguswa yanazungumziwa kana kwamba yalikuwa kichafu kimaumbile.

kilichosafi

Mtu au kitu ambacho Yahweh amekitamka kuwa hakifai kuguswa yanazungumziwa kana kwamba yalikuwa safi kimaumbile.

Leviticus 10:12

sadaka ifanywayo kwa Yahweh kwa moto

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Sadaka za kuteketezwa kwa Yahweh"

kwa kuwa ni takatifu sana

"kwa kuwa sadaka ya nafaka ni takatifu sana"

hivi ndivyo nimeamriwa kuwaambia ninyi

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa tendakji. : "hivi ndivyo Yahweh ameniamru kuwaambia ninyi"

Leviticus 10:14

Kile kidari kitikiswacho na lile paja ambalo hutolewa kwa Yahweh

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "kile kidali na paja ambalo mtu alilitikisa na kuipeleka kwa Yahweh"

kidari

ile sehemu ya mbele ya mwili wa mnyama chini ya shingo

paja

ile sehemu ya juu mguu juu ya goti

Wewe mwenyewe, wanao na binti zako

"Wewe" hapa humaanisha Aroni

Nazo zitakuwa zako wewe na wanao uwe mgao wenu daima

Hii ijulikane kwamba sehemu hiyo ni ya Aroni na wanawe. : "Sehemu hii daima itakuwa kwa ajili yako na wanao"

Leviticus 10:16

ametekezwa kwa moto

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Kuhani alikuwa ameiteketeza yote"

Eleazari and Ithamari

Yafasiri majina haya kama yalivyofasiriwa katika sura ya 10:5

Kwa nini hamjaila ... mbele zake?

Musa anatumia swali kuwakemea Eleazari na Ithamari. swahili hili lenye ufsaha laweza kufasiriwa tamko. : "Iliwapasa kuwa mmeila...mbele zake."

kwa kuwa ni takatifu sana

"kwa kuwa sadaka ya dhambi ni takatifu sana"

kuchukua uovu wa kusanyiko

Ikimsababisha Yahweh kuwasamehe watu wa Israeli kunazungumziwa kana kwamba uovu ulikuwa kitu ambacho Yahweh hukichukua kutoka kwa watu.

mbele zake

"katika uwepo wake"

Tazama, damu yake haikuletwa ndani ya hema

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "hukuileta damu yake"

Leviticus 10:19

jambo hili vilevile limetendeka kwangu

Aroni anarejea kwa kifo cha wanawe wawili.

Isingekuwa imeshapendeza mbele za Yahweh?

Dhabihu hizi zilikuwa za kuliwa kwa shangwe na furaha. Aroni anatumia swali kusisitiza kwamba Yahweh asingekuwa amependezwa naye kwa kula dhabihu kwa kuwa anahuzuni kwa sababu ya vifo vya wanawe. Swali hili laweza kufasiriwa kama tamko. : "hakika Yahweh asingekuwa amependezwa."

Leviticus 11

Leviticus 11:1

miongoni mwa wanyama

"kutoka kwa wanyama wote"

Leviticus 11:3

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile anawachoruhusu watu kula na kile ambacho anawazuia kula.

kwato zenye kugawanyika

Hii humaanisha kwamba kwato zilizogawanyika sehemu mbili badala ya kuwa wayo mmoja

hucheua.

Hii humaanisha mnyama anayeleta chakula kinywani kutoka tumboni mwake na hukitafuna tena.

aadhi ya wanyama ambao ama hawacheui au hana kwato zilizogawanyika

Yaani kwamba, wana moja au nyingine, lakini siyo yote mawili.

ngamia ni najisi kwenu

Ngamia kuwa hafai kwa watu kumla amaezungumziwa kana kwmaba alikuwa mchafu kimaumbile.

Leviticus 11:5

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwambia Musa na Aruni kile anachowaruhusu watu kula na kile ambacho anawakataza kula.

Pimbi

Mnyama mdogo aishiye maeneo ya miamba.

najisi kwenu

wanyama hawa ambao Mungu amewatamka hawafai kwa watu kuwala wamezungumziwa kana kwamba walikuwa wachafu kimaumbile.

Sungura

Mnyama mdogo mwenye manyoya marefu ambaye kwa kwaida huishi kwenye mashimo chini ardhini.

wala msiiguse mizoga yao

"wala msiguse miili yao iliyokufa"

Leviticus 11:9

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwambia Musa na Aruni kile anachowaruhusu watu kula na kile ambacho anawakataza kula

Mapezi

pezi , ni sehemu iliyobapa ambayo samaki huitumia kuogelea majini.

Magamba

Ni mabamba madogo madogo yanayoufunika mwili wa samaki.

viumbe wote hai wasio na mapezi na magamba waliomo baharini au mitoni

"wanyama wote waishio baharini au mitoni wasio na mapezi na magamba"

watakuwa chukizo kwenu

Yahweh anawaamru watu kuwakataa na kudharau kuwal a viumbe hawa. Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yapsa mwawachukie hao" au "lazima mukatae kabisakabisa"

Leviticus 11:11

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwambia Musa na Aruni kile anachowaruhusu watu kula na kile ambacho anawakataza kula

Kwa kuwa watakuwa chukizo

"kuchukia" ni kukitaa na kukidharamu kitu. Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo" wa utendaji. : "kwa kuwa yawapasa kuwachukia hao au kwa kuwa ni lazima muwakatae kabisakabisa"

mizoga yao sharti itakuwa chukizo

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ywapasa kuichukia miili yao iliyokufa" au "msiguse miili yao iliyokufa"

Chochote kisichokuwa na mapezi au magamba kilichomo majin

"Chocote kilichomo majini kisichokuwa na mapezi na magamba"

lazima kiwe chukizo kwenu

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "lazima mvichukie" au "lazima mvikatae kabisa kabisa"

Leviticus 11:13

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwambia Musa na Aruni kile anachowaruhusu watu kula na kile ambacho anawakataza kula

tai, furukombe, kipungu, mwewe mwekundu, aina yoyote ya kipanga, kila aina ya kunguru, 16kiruka-njia, kipasuasanda, Shakwe..aina yoyote ya mwewe.

Kuna ndege ambao ama hukaa macho usiku au hula panya na wanyama waliokufa.

Leviticus 11:17

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwambia Musa na Aruni kile anachowaruhusu watu kula na kile ambacho anawakataza kula

bundi mdogo...bundi mkubwa...chukizo, mnandi, bundi mweupe na mwari, korongo...ina zote za koikoi, huduhudi...popo

Hawa ndege walao panya na wadudu na aghalabu hukaa macho usiku

bundi mkuu

""bundi mkubwa"

Koikoi...huduhudi

Hawa ni ndege walao panya na mijusi.

popo

Ingawaje popo si ndege, kwenye orodh hii popo ni najisi kwa sababu ana mabawa na huruka. ana mwili wa manyoya na hasa hukaa macho usiku. Yeye hula wadudu na panya

Leviticus 11:20

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwambia Musa na Aruni kile anachowaruhusu watu kula na kile ambacho anawakataza kula

Wadudu wote wenye mabawa wanaotembea kwa miguu minne ni machukizo kwenu

Neno hili "chukuzo" laweza kufasiriwa na kirai che kitenzi. : "Mtawachukia wadudu wote wenye mabawa wanaotembeao kwa miguu yao miine"

Wadudu watembeao kwa miguu minne

Kirai "miguu miine" hapa ni nahau inayomaanisha kutambaa juu ya ardhi na huwatenga wadudu hawa na vitu vingine virukavyo, kama vile ndege, ambao wana miguu miwili tu. : "wadudu wataambao juu ya ardhi"

nzige, senene, parare, au panzi.

Hawa ni wadudu wadogo ambao hula mimea na wanaweza kurukaruka.

wadudu warukao wenye miguu minne

"wadudu warukao walio na miguu miine"

Leviticus 11:24

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaanza kuwaambia Musa na Aroni ni wanyama gani ambao watu wanatakiwa kuwaona najisi.

Nanyi mtakuwa najisi hata jioni kutokana na wanyama hawa endapo mtagusa mizogo yao

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Miili ya wanya wanyama hawa waliokufa itawafanya nyinyi kuwa najisi kama mtagusa mmojawapo.

mtakuwa najisi

Mtu asiyekubalika kwa kusudi la Mungu kwa sababu amegusa mojawapo ya miili ya wanyama waliokufa anazungumziwa kana kwamba amekuwa si mchafu kimaumbile.

wanyama hawa

Hii hurejelea wanyama anaotaka kuwaorodheshaa katika mistari inayofuata.

Leviticus 11:26

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwambia Musa na Aruni kile anachowaruhusu watu kula na kile ambacho anawakataza kula

Kila myama...ni najisi kwenu

Hawa wanyama ambao Mungu amewataja kutofaa kwa kuliwa na watu wamezungumziwa kana kwamba walikuwa wachafu kimaumbile.

kwato zilizogawanyika

Tazama amelezo ya sura ya 11:3.

Cheuwa

Tazama maelezo ya sura ya 11:3

Kiala awagusaye atakuwa najisi

Mtu ambaye hakubaliki kwa makusudi ya Mungu kwa sababu ya amegusa mmojawapo wa wanyama hawa anazungumziwa kana kwamba alikuwa mchafu kimaumbile.

vitanga

Miuguu ya mnyama yenye makucha

hata jioni

"hata macheo"

Leviticus 11:29

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwambia Musa na Aruni wanyama ambao watu walitakiwa kuwaona najisi

hawa ndiyo walio najisi kwen

Hawa wanyama ambao Mungu amewataja kuwa hawafai kuguswa au kuliwa na watu wamezungumziwa kana kwamba walikuwa wachafu kimaumbile

kicheche

mnyama mdogo mwenye manyoya ya kahawia anayekula ndege na wanyama wadogo.

mijusi mikubwa, guruguru, 30kenge, mijusi ya ukutani...na kinyonga

Hizi ni aina mbali mabali za wanyama wenye damu baridi walio na miguu minne.

goromoe

"Mjusi wa ni"

Leviticus 11:31

Taarifa kwa Ujmla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aruni wanyama ambao watu walitakiwa kuwaona najisi

hawa ndiyo watakuwa najisi kw

Hawa wanyama ambao Mungu amewataja kuwa hawafai kuguswa au kuliwa na watu wamezungumziwa kana kwamba walikuwa wachafu kimaumbile

Yeyeote awagusaye...atakuwa najisi

Mtu ambaye hakubaliki kwa makusudi ya Mungu kwa sababu amegusa mmojawapo wa wanyama hawa anazungumziwa kana kwamba alikuwa mchafu kimaumbile

hata jioni

"hata macheo"

chombo hicho kitakuwa najisi

Chombo amacho Mungu amekitaja kuwa hakifai kwa watu kukigusa kwa sababu mwili wa mmojawapo wa myama hawa aliyekufa umeangua juu yake kimezungumziwa kana kwamba klikuwa kichafu kimaumbile. Kimezungumziwa kufaa baada ya kuwa kimeoshwa.

Kisha kitakuwa safi.

Kitu flani ambacho Mungu amekitaja kuwa kinafaa kwa watu kukiguza baada ya kuwa kimeoshwa kimeangumziwa kana kwamba kilikuwa safi kimaumbile.

lazima kitalowekwa katika maji

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "na vyovyote utakavyokitumia, itakupasa kukiloweka kwenye maji.

Leviticus 11:34

Vyakula vyote ambavyo ni safi

Vyakula ambavyo Mungu amevitaja kuwa vimekubalika kwa watu kula kimezumgumziwa kana kwamba kilikuwa safi kimaumbile.

na kilichoruhusiwa kuliwa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ambacho waweza kukila"

.nacho kitakuwa najisi

Chakula kisichokubalika kwa watu kukila kwa sababu maji yaliyonajisi yamemwagikia juu yake kimezungumziwa kana kwamba kilikuwa kichafu kimaumbile

kinachoweza kunywewa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "waweza kunywa"

cha mzoga

"cha maiti"

Ni lazima kivunjwevunjwe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Ni lazima ukivunje vipandevipand"e au "Yakupasa kukisambaratisha"

Leviticus 11:36

Taariifa kwa Ujumla

Yahweh anaendele kuwaambia Musa na Aroni ni wanyama gani ambao watu waahesabu najisi

Chemchemi au kisima...patabaki kuwa safi

Maji yale ambayo watu wameruhusiwa kunywa kutoka chemchemi au kisima yanapokusanyika pamezungumziwa kana kwamba palikuwa safi kimaumbile.

kisima cha maji ya kunywa yanapokusanyika

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Kisima kinachokusanya maji ya kunywa"

mzoga wa mnyama aliye najisi

maiti ya mnyama ambaye Mungu amamtaja kuwa hafai kwa watu kumgusa au kumla amezungumziwa kana kwamba alikuwa mchafu kimaumbile

yeye atakuwa najisi

Yule mtu asiyekubalika kwa kusudi la Mungu kwa sababu kagusa mzogo wa mmojawapo wa wanyama amazungumziwa kana kwamba alikuwa mchafu kimaumbile.

mbegu...kwa ajili ya kupanda

"mbugu ambazo mnatarajia kupanda"

Mbegu hizo zitakuwa bado zingali safi...zitakuwa najisi

Mbegu ambazo Mungu amezitaja kuwa zimekubalika kwa watu kupanda zimezungumziwa kana kwamba zilikuwa safi kimaumbile na zile ambazo hazikubaki zimezungumziwa kana kwamba zilikuwa chafu

Lakini kama maji yanawekwa juu ya mbegu

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. "Lakini kama mtaweka juu ya mbengu"

Leviticus 11:39

naye yeyote amgusaye atakuwa najisi hata jioni

Tazama maelezo ya sura ya 11:31

Hata jioni

Hata machweo

Leviticus 11:41

atakua chukizo

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yapasa mmchukie" au "yapasa mkatae"

Taariifa kwa Ujumla

Yahweh anaendele kuwaambia Musa na Aroni ni wanyama gani ambao watu waahesabu najisi

hatakuwa wa kuliwa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Haipasi kumla"

watakuwa machukizo.

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yawapasa kuwachukia" au "Lazima muwakate"

Leviticus 11:43

Taariifa kwa Ujumla

Yahweh anaendele kuwaambia Musa na Aroni ni wanyama gani ambao watu waahesabu najisi

Msijitie unajisi... msije mkachafuliwa navyo.

Yahweh anarudia wazo lilelile mara mbili ili kutia nguvu amri kwamba haiwapasi kula mnyama yeyote aliyenajisi.

msijitie unasi kwavyo

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "kiasi kwamba mnakosa kuwa safi kwa sababu ya hivyo"

Leviticus 11:46

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anamaliza kuwaambia Musa na Aroni kile anachowaruhusu watu kula na kilea nachowakataza kula.

kwa jili ya kile kinachopaswa kutofautishwa kati

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. :"kwa ajili ya kupambanua baina ya"

kutofautishwa kati ya kilicho najisi na kilicho safi

Wale wanyama ambao MUngu aliwataja kuwa hawafai kwa watu kuwa gusa au kuwala wamezungumziwa kana kwamba walikuwa wachafu kimaumbile, nwa wale aliowataja kukubalika kwa watu kuwagusa na kuwala wamezungumziwa kana kwamba walikuwa wasafi kimaumbile.

ambavyo vyaweza...visivyoweza kuliwa."

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ambacho mwaeza kula...amcho hamwezi kula"

Leviticus 12

Leviticus 12:1

naye atakuwa najisi

Mwanamke ambaye watu wengine haiwapasi kumgusa kwa sababu anatokwa ujauzito wake anazungumziwa kana kwamba alikuwa najisi kimaumbile.

katika siku za kipindi chake kwa mwezi

Hii hurejealea kipindi cha mwezi mwanamke anapotokwa na kutokana na ujauzito wake.

nyama ya govi la mtoto mvulana itatahiriwa

Ni kuhani tu pekee angeweza kufanya tendo hili. Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "kuhani ndiye apaswaye kumtahiri mtoto mvulana"

Leviticus 12:4

utakaso wa mama wa kutokwa damu yake utaendelea kwa muda wa siku thelathini na tatu

Siku tatu - Hii humaanisha kwmba mama atabakia najisi kwa siku sitini na tatu.

muda wa thelathini na tatu

siku tatu - "siku 33"

naye atakuwa najisi kwa muda wa majuma mawili

Mwanamke ambaye watu wengiine haiwapasi kumgusa kwa sababu anatokwa damu kutokana na mimba yake amezungumziwa kana kwamba alikuwa mchafu kimaumbile.

kwa mud wa majuma mawili

"kwa siku 14"

wakati wa kipindi chake

Tazama maelezo ya sura ya 12:1

siku sitini na sita

siku sita - "siku 66"

Leviticus 12:6

Siku za kutakaswa kwake zitakapomalizika

Siku za mwezi za utakaso wake zitakapokamilika"

kwa ajili ya mwana au bint

Hii hurejelea idadi tofauti ya siku za utakaso kutegemeana na jinsia ya mtoto anayemzaa; mwana au binti.

Leviticus 12:7

naye atatakaswa kutokana kutiririka kwa damu yake

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "na hili litamtakasa kutoka katika kutokwa na damu kwake kunaoendelea wakati wa kuzaliwa kwa mtoto.

kama hana uwezo wa kutoa mwana-kondoo

Fasiri sentensi hii ili kuweka wazi kutokuweza kwa mwanamke kununua dhabihu ya mnyama. : "Iwapo hana fedha ya kutosha kukunulia mwana-kondoo"

naye atakuwa safi

Mwanamke ambaye watu wengine wangeweza kumgusa anazungumziwa kana kwamba alikuwa safi kimaumbile.

Leviticus 13

Leviticus 13:1

lazima aletwe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "kisha yapasa mmoja kumleta yeye" au "kisha yapasa yeye aende"

kwa mmoja wa wanawe

"kwa mmoja wa watoto wa Aroni"

Leviticus 13:3

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni juu ya kile watu wafanye.

ngozi ya mwili wake

"Wake" hapa humrejelea mtu mwenye ugonjwa wa ngozi.

ugonjwa wa kuambukiza

ugonjwa ambao unaweza kuenea kwa urahisi kutoka kwa mtu mmoja hadi kwa mwingine.

atamtangaza kuwa ni najisi

"ni lazima kuhani amtangaze najisi mtu huyo." Mtule yule ambaye watu wengine hawapaswi kungusa amezungumziwa kana kwamba alikuwa mchafu kimaumbile.

kwa siku saba.

"kwa siku 7"

Leviticus 13:5

huyo kuhani itambidi kumchunguza

Anayechunguzwa hapa ni yule mtu aliye na ugonjwa wa ngozi

kama haujaenea kwenye ngozi

Hii inamaanisha kwamba kama ugonjwa wa ngozi haujaongozeka katika ukubwa au haujasogea kwenye sehemu zingine za mwili.

siku ya saba

"Ya saba" ni idadi kwa 7. : "siku ya 7"

siku saba

"Siku 7"

Naye kuhani atamtangaza safi ...yeye ni safi.

Yule mtu ambaye wengine wangemgusa amezungumziwa kana kwamba ni safi kimbaumbile.

upele

Hii ili eneo la ngozi lililoumbuliwa, lakini upele upele hataenea kwa watu wengine.

Leviticus 13:7

amejionyesha

Hii hurejea moja kwa moja kwa mtu aliye na ugonjwa wa ngozi.

kuhani atamtangaza kuwa najisi

Yule mtu ambaye watu wengine haiwapasi kumgusa amezungumziwa kana kwamba alikuwa mchafu kimaumbile

ugonjwa wa kuambukiza

Tazama maelezo ya sura 13:3.

Leviticus 13:9

huyo yapasa aletwe kwa kuhani

Kuhani aliamua iwapo ugonjwa ulikuwa umesambaa. Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "mmoja nanweza kumleta kwa kuhani" au "anapaswa kumwendea kuhani"

endapo...kumekuwa na nyama mbichi kwenye uvimbe.

"Nyama mbichi" hapa inaweza kumaanisha vidonda vilivyowazi juu ya ngozi au yaweza kumaanisha ngozi mpya imemea, lakini eneeo kukizunguka badao inaugonjwa. ama mojawapo inanyesha kwamba ugonjwa wa ngozi yenye hauponi sawasawa.

ugonjwa sugu wa ngozi

Huu ni ugonjwa ambao au unapona kwa muda wakati mrefu.

naye kuhani atamtangaza kuwa najisi...yeye tayari ni najisi

Yule Mungu ambaye watu wengine hawapasi kumgusa anazungumziwa kana kwamba alikuwa mchafu kimaumbile.

Leviticus 13:12

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni yawapasayo watu kufanya mtu anapokuwa na ugonjwa wa ngozi.

kuhani atamtangaza mtu huyo...safi...naye atakuwa safi

Mtu ambaye watu wengine wanaweza kumgusa amezungumziwa kana kwamba alikuwa safi kimaumbile na mtu ambaye watu wengine haiwapasi kumgusa amezungumziwa kana kwamba alikuwa mchafu kimaumbile.

Leviticus 13:15

Kuhani atamtangaza...najisi kwa sababu hiyo nyama yake mbichi ni najisi

Tazama maelezo ya hapo juu 13:6

kumtangaza kuwa najisi

Anayetangazwa hapa ni yule mwenye ugonjwa wa ngozi

nyama mbichi

Tazama mafafanuzi yaliyo kwenye 13:9

ugonjwa wa kuambukiza

Imefasiriwa kama ilivyofanyika katia 13:3

kuhani atatangaza kwamba mtu huyo kuwa safi

Yule mtu ambaye watu wengine wanaweza kumgusa amezungumziwa kana kwamba akuwa safi kimaumbile.

Leviticus 13:18

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu inawapasa kufanya mtu anapokuwa na ugojwa wa ngozi.

Jipu

Eneo juu ya ngozi iliyoambukizwa lenye maumivu makali.

yapasa kuonyeshwa kwa kuhani.

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yapasa alionyeshe kwa kuhani"

kuhani atamtangaza kuwa najisi

Mtu ambaye watu wengine haiwapasi kumgusa amezungumzwa kana kwamba alikuwa mchafu kimaumbile.

Leviticus 13:21

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu inawapasa kufanya mtu anapokuwa na ugojwa wa ngozi.

analichunguza

Kinachochunguzwa hapa ni ule uvimbe au doa ling'aalo juu ya ngozi.

kuhani atamtangaza kuwa najisi.

Tazama maelezo ya sura ya 13:20

naye kuhani atamtangaza kuwa safi

Mtu ambaye watu wengine wanaweza kumgusa amezungumziwa kana kwamba alikuwa safi kimaumbile.

Leviticus 13:24

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu inawapasa kufanya mtu anapokuwa na ugojwa wa ngozi.

Ugonjwa wa kuambukiza

Tazama maelezo sura ya 13:3

naye kuhani atamtangaza kuwa najisi

Tazama maelezo ya sura 13:20

Leviticus 13:26

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu inawapasa kufanya mtu anapokuwa na ugojwa wa ngozi.

analichunguza

Kinachochunguzwa hapa ni lile jeraha la moto juu ya ngozi ya mtu.

naye kuhani atamtangaza kuwa najisi

Tazama amaelezo ya sura 13:20

Ugonjwa wa kuambukiza

Tazama maelezo ya sura 13:3

, naye kuhani atamtangaza kuwa safi

Tazama maelezo ya sura 13:23

Leviticus 13:29

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu inawapasa kufanya mtu anapokuwa na ugojwa wa ngozi.

kuhani atamtangaza kuwa najisi

Tazama maelezo ya sura 13:20

Leviticus 13:31

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu inawapasa kufanya mtu anapokuwa na ugojwa wa ngozi.

Leviticus 13:32

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu inawapasa kufanya mtu anapokuwa na ugojwa wa ngozi.

basi, yapasa mtu huyo kunyolewa., lakini sehemu yenye ugonjwa haitanyolewa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "mtu huyo atalazimika kunyoa nywele zilizokaribu na jipu lakini siyo zile nywele zilizojuu ya jipu"

Leviticus 13:34

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu inawapasa kufanya mtu anapokuwa na ugojwa wa ngozi.

ule ugonjwa

"Ugonjwa" hapa humaanisha ule ugonjwa juu ya kichwa au kidevu cha mtu.

kuhani atamtangaza kuwa safi. Mtu huyo yapasa kufua nguo zake, na kisha atakuwa safi

Tazama maelezo ya sura 13:23

Leviticus 13:35

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu inawapasa kufanya mtu anapokuwa na ugojwa wa ngozi.

baada ya kuhani kutangaza kuwa alikuwa safi...Yeye ni safi, naye kuhani atamtangaza safi

Tazama maelezo ya sura 13:23

Mtu huyo ni najisi

Tazama maelezo ya sura 13:20

Leviticus 13:38

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu inawapasa kufanya mtu anapokuwa na ugojwa wa ngozi.

meupe kwa kufifia

kovu jeupe

Kovu

Tazama maelezo ya 13:5

Yeye yu safi.

"Mtu huyo yu safi"

Yeye yu safi.

Tazama maelezo ya sura 13:23

Leviticus 13:40

aelezo kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu inawapasa kufanya mtu anapokuwa na ugojwa wa ngozi.

yeye yu safi

Tazama maelezo ya sura 13:23

Leviticus 13:42

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu inawapasa kufanya mtu anapokuwa na ugojwa wa ngozi.

Ugonjwa wa kuambukiza

Tazama maelezo ya sura 13:3

naye ni najisi...atamtangaza kuwa najisi

Tazama maelezo ya sura 13:20

Leviticus 13:45

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu inawapasa kufanya mtu anapokuwa na ugojwa wa ngozi.

nje ya kambi

Kambi ni eneo ambao Waisraeli wengi wailiishi. Mtu najisi alikuwa haruhusiwi kuishi miongoni mwao kwa sababu ugonjwa wake unaweza kuenea kwa wengine.

Najisi, najisi

Tazama aelezo ya sura 13:20

Leviticus 13:47

vazi la mtu huchafuliwa na ukungu

"Vazi lenye ukungu juu yake" au Vazi ambalo linaukungu"

kuchafuliwa

Kuwa chafu kwa sababukitu fulani chenye madhara kimeongezwa kwake.

ukungu

Kuvu, mala kwa mara huwa na rangi nyeupe, ambayo hukua juu ya vitu vilivyovichafu au vyenye unyevunyevu

au kitu chochote kilichosukwa au kufu

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji' : : "au kitu chochote ambacho mtu aliye amekisokota au kukisuka"

Iwapo sehemu iliyochafuliwa ina rangi ya kijani au nyekundu katika vazi

"kama kuna uchafu wa kijani au wenye wekundo kwenye vazi"

kitu chochote kilichotengenezwa kwa ngozi

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "kitu chochote kile ambacho mtu amekitengeneza kutoka na na ngozi"

lazima kionyeshwe kwa kuhani

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Mmiliki wake yapasa kukionyesha kwa kuhani"

Leviticus 13:50

siku saba

Tazama maelezo ya sura 13:5

siku ya saba

Tazama maelezo ya sura 13:6

kitu chochote ambacho ngozi imetumika

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "kitu chochote ambacho mtu anatumia ngozi"

kifaa chochote kilichoonekana na ukungu ndani yake

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Chochote ambacho kinapatika na ukungu wenye kudhuru juu yake"

kifaa hicho ni najisi

Maelezo yake yaweza kufanana na ya sura 13:20

huo ukungu unaweza kusababisha ugonjwa

Huo ukungu wenyekudhuru waweza kusababisha ugonjwa ndani ya mtu anayekikaribia kifaa.

Chombo hicho lazima kiteketezwe kabisa kwa moto

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yapasa akiteketeze hicho chombo kabisakabisa

Leviticus 13:53

basi atawaamru

"kisha kuhani atamwamru mmiliki" Hapa kuhani anawaambia watu namna ya kuvitendea vyombo vya nymbani ambavyo yamkini vilikuwa vimembukizwa.

hicho kifaa kilichopatikana na ukungu

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ambamo wamegundua mna ukungu"

baada ya kuwa kimesafishwa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "baada ya kukiosha kifaa"

kifaa hicho ni najisi

Kitu ambacho Mungu amekitangaza kuwa hakifai kwa watu kukigusa kimezungumziwa kana kwamba kilikuwa kichafu kimaumbile.

Yapasa ukichome kifaa hicho

"ukichome" hapa haimaanishi kuhani hasa. Inamaanisha tu mtu impasaye kukichoma kifaa.

Leviticus 13:56

baada ya kuwa umeoshwa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Baada ya miliki kuwa amekiosha"

lazima utakichoma moto

Anayelazimika hapa haimaanishi kuhani hasa. bali inamaanisha tu yule anayepaswa kukichoma hicho chombo.

iwapo unakisafisha kifaa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : Endapo mmiliki anakiosha"

nao ukungu ukawa umetoka, nacho kifaa lazima kisafishwe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "kisha huyo mmiliki lazima akioshe"

kisha kitakuwa safi.

Tazama maelezo ya sura 13:23

Leviticus 13:59

ukungu katika vazi....lilotengenezwa kwa ngozi

Tazama linavyofasireiwa katika sura 13:47

ili kwamba mweze kuvitangaza

"ili kwamba kuhani aweze kukitangaza"

safi au najisi

Tazama maelezo ya sura 13:20-23

Leviticus 14

Leviticus 14:1

Maelezo kwa Ujumla

Yahweh aHii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji.nawaambia Musa na Aroni kile ambacho watu wanapaswa kufanya mtu anapotakaswa ugonjwa wa ngozi.

siku yake ya utakaso

Hii hurejelea siku ya ambayo kuhani anamtangaza mtu kuwa ni safi kwa kanuni za kidini

Ni lazima aletwe kwa kuhani

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Mtu mmoja anaweza kumleta kwa k"uhani au "Yeye anaweza kwenda kwa kuhani"

Leviticus 14:3

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendele kuwaambia Musa na Aroni ambacho watu wafanye mtu anapotakaswa ugonjwa wake wa ngozi.

madhara ya ugonjwa wa ngozi

Tazama maelezo ya sura ya 13:3

mtu wa kutakaswa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Mtu anayemtakasa"

ndege safi

Tazama maelezo ya sura ya 13:23

kitani nyekundu

"uzi mwekundo"

Leviticus 14:6

Taarifa kwa Ujumla

Tazama maelezo ya sura 14:3

ndege aliyechinjiwa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Ndenge ambaye mtu alimuua"

mtu ambaye amekuwa akitakaswa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "mtu anayemtakasa"

atamtangaza kuwa safi

Tazama maelezo ya sura 13:23

Leviticus 14:8

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anawaambia Musa na Aroni kile ambacho watu wafanye mtu anapotakaswa ugonjwa wa ngozi

ambaye amekuwa akitakasw

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Mtu ambaye kuhani anamtakasa"

naye atakuwa safi

Tazama maelezo ya sura 13:23

Leviticus 14:10

itambidi kuchukua

Hapa anayepaswa kuchukua ni yule aliyetakaswa.

efa

Efa moja ni sawasawa na lita 22.

logi

Logi moja ni sawasawa na lita 0.31

yeye atakaswaye

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "mtu anayemtakasa"

Leviticus 14:12

Logi

Logi mmoja ni sawasawa na lita 0.31

katika eneo la hema

Kirai hiki kinafafanua kirai kilichotangulia na kutoa maelezo zaidi juu ama kuhani aliyekuwa amchinje huyo mwana-kondoo

Leviticus 14:14

mtu wa kutakaswa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "mtu anayemtakasa"

Logi

Logi moja ni sawasawa na lita 0.31

kunyunyiza sehemu ya mafuta...mbele za Yahweh.

"kunyunyizia sehemu ya mafuta... mbele za Yahweh" hakuna kiashiria cha kile ambacho kuhani alinyinyizia mafuta juu yake.

Leviticus 14:17

mafuta yaliyobaki mkononi mwake

"mafuta yaliyobaki yaliyomo mkononi mwake

Mtu anayetakaswa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : " mtu anayemtakasa"

mbele za Yahweh

"katika uwepo wa Yahweh"

Leviticus 14:19

yake yeye wa kutakaswa

Hii yaweza kufasiriwe katika mtindo wa utendaji. : "mtu anayemtakasa"

naye atakuwa safi

Tazama maelezo ya sura 13:23

Leviticus 14:21

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu wanapaswa kufanya mtu anapotakaswa ugonjwa wa ngozi.

hawezi kumudu

"hana fedha ya kutosha kununua"

kutikiswa...kwa ajili yake

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ambaye kuhani atamtikisa...kwa ajili ywke"

moja ya kumi ya efa

kumi ya efa ni - moja ya kumi ya efa ni swaswa na lita 22.

Logi

Logi moja ni swasawa na lita 0.31

Leviticus 14:24

Logi

Logi moja ni swasawa na lita 0.31

anayemtakasa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yule anayemtakasa"

Leviticus 14:26

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu wanapaswa kufanya mtu anapotakaswa ugonjwa wa ngozi.

sehemu ya mafuta...atanyunyizia...mbele za Yahweh

"sehemu ya mafuta...nyunyizia...mbele za Yahweh." Hakuna kiashiria cha kile ambacho kuhani aliyanyunyizia mafuta juu yake.

Leviticus 14:28

yule wa kutakaswa

Tazama maelezo ya sura 14:19

Leviticus 14:30

Atatoa

"Kuhani atatoa"

yule wa kutakaswa

Tazama ameleo ya sura 14:19

Ugonjwa wa kuambukiza

Tazama maelezo ya sura 13:3

asiye mudu

: "asiyekuwa na fedha ya kuutosha kuweza kununua"

Leviticus 14:33

Mtakapoingia

"mtakapoingia" hapa inamaanisha watu wa sraeli.

ukungu

Tazama maelezo ya sura 13:42

katika nchi ya milki yenu

Neno "milki" laweza kufasiriwa kama kitenzi. : "katika nchi mnayoimiliki"

Leviticus 14:36

ili kwamba kusiwe na kitu ndani ya nyumba kitakachonajisika

mara tu kuhani alipoitangaza nyumba najis, kila kitu kilichokuwa kwenye nyumba kilikuwa najisi pia. Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "kiasi kwamba hahitaji kutangaza kitu cho chote kilichosalia ndani ya nyumba kuwa najisi"

ndani ya nyumba kitakachonajisika

Tazama maelezo ya sura 13:20

katika bonde za kuta.

Hii inamaanisha kwamba kuhani ndiye atakayeamua iwapo ukungu umeingi ndani ya nyuso za kuta tu.

Leviticus 14:39

ambayo kwayo ukungu umepatikana

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ambamo ukungu liuona"

mahali palipo najisi

Tazama maelezo ya sura 13:20

Leviticus 14:41

Naye atataka

"Naye" hapa humaanisha kuhani.

zikwanguliwe kuta zote za ndani ya hiyo nyumba

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "kwamba mmiliki anazikwangua kuta zote za nadani"

vilivyochafuliwa na hivyo vifaa vilivyokwanguliwa

Hii humaanisha vifaa vyenye ukungu juu yake. Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : KIfaa kilichochafuliwa kile walichokikwangua"

mahali paliponajis

Tazama maelezo ya 13:20

mawe yaliyoondolewa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yale mawe waliyoyaondoa"

lazima watumie udongo mpya kuipiga lipu hiyo nyumba

"lazimz wayafunike hayo kwa udongo mpya"

Leviticus 14:43

katika nyumba...na kupigwa lipu upya

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "katika nyumba baada ya mmiliki kuyaondoa mawe, amezikwangua kuta, na kuyafunika mawe kwa udongo.

nyumba hiyo ni najisi

Taama maelezo ya sura 13:20

Leviticus 14:45

Yapasa hiyo nyumba ibomolewe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yapasa waiangushea nyumba chini"

Na hayo mawe, na udongo wa lipu vitachukuliwa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yapasa waondowe mawe, mbao, na lipu yote katika nyumba"

yeyote aingiaye ndani ya nyumba....atakuwa najis

Tazama maelezo ya sura ya 13:20

hata jioni

"mpaka machweo"

Leviticus 14:48

nyumba kuwa imepigwa lipu

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "mmiliki anaweka udongo mpya juu ya nyumba"

ndipo atatangaza kuwa nyumba hiyo ni safi

Tazama maelezo ya sur 13:23

Leviticus 14:49

mti wa mwerezi , hisopo, kitambaa chekundu ... damu ya ndege aliyeuawa

Tazama maelezo ya sura ya 14:3

damu ya ndege aliyeuawa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ile damu ya ndege ambaye yeye limuua"

Leviticus 14:52

Atalitakaza nyumba

"Kuhani ataifanya safi nyumba kwa kawaida za kidini"

nayo itakuwa safi

Tazama maelzo ya sura 13:23

Leviticus 14:54

athari ya ugonjwa wa ngozi

Tazama maelezo ya sura13:3

Ukungu

Tazama maelezo ya 13:47

vipele

Tazama amelezo ya sura 13:5

najisi...safi

Tama maelezo ya sura13:20 na 23

Leviticus 15

Leviticus 15:1

unaotoka mwilini mwake

Hii hurejelea semhemu nyeti za mtu.

huwa najis

Tazama maelezo ya sura 13:20

ni najisi

"mwili wake ni najisi" au "yeye ni najisi"

Leviticus 15:4

najisi

Tazama maelezozo ya sura 13:20

Yeyote agusaye kitanda....na atakuwa najisi

Tazama maelezo ya sura ya 13:23

Hata jioni

Mpaka machweo.

Leviticus 15:6

naye atakuwa najisi

Tazama maelezo ya sura 13:20

hata jioni

"paka machweo"

agusaye mwili

"yeye agusaye sehemu yoyote ya mwaili"

Leviticus 15:8

mtu mwingine aliyesafi

Tazama maelezo ya sura 13:23

atakuwa najisi

Tazama maelezo 13:20

Tandiko

Tandiko ni kiti cha ngozi ambacho mtu hukiweka mgongoni mwa farasi ili kumpanda aende safari

Tandiko lolote...litakuwa najisi

Tazama maelezo ya sura 13:20

Leviticus 15:10

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kiwapasacho watu kutenda ili kuzuia maabukuizi.

mtu huyo

Hii humrejelea mtu aliye maambukizi ya ugiligili.

atakuwa najisi

Tanzama maelezo ya sura 13:20

hata jioni

"mpaka macheo"

Yeyote yule aliye na mtiririko kama huo anamgusa

Yeyote aguswaye na mtu mwenye mtiririko"

Chungu chochote cha udongo anachokigusa mwenye kutiririkwa na ugiligili kama huo yapasa kivunjwe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Mtu yeyote anaweza kuweza kukuvunja chungu chochote cha udongo ambacho amekigusa mtu mwenye mtirirko kama huo"

kila chombo cha mti lazima kisafishwe kwenye maji

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ni lazima mtu asuuze kwenye maji kila chombo cha mbao"

Leviticus 15:13

anapotakaswa kutoka kwnye kutiririkwa kwake

Tazama maelezo ya sura 13:23. Na hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "aponapo kutka kwenye kutiririka kwake"

Naye atakuwa safi

Tazama maelezo ya sura 13:23

Leviticus 15:16

najisi hata jioni

Tazama amelezo ya 13:20

hata jioni

"mpaka macheo"

Kila vazi...lazama ifuliwe kwa maji

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Mtu atalazimika kufua kila vazi au ngozi ambayo juu yake kuna shahawa

Leviticus 15:19

hedhi...kipindi chake

Haya yote mawili hurejelea kwenye kipindi cha kutirirka kwa damu kutoka kwenye tumbo la mwanamke.

uchafu kutengwa kwake kutaendelea

"ataendelea kuwa mchafu"

kitakuwa najisi

Yazama maelezo ya sura 13:20

Leviticus 15:21

Kitanda chake

Hii humrejelea mwanamke aliyeingia damuni"

mtu huyo atakuwa najisi

Tazama maelezo ya sura 13:23

Hata jioni

"mpaka macheo"

Leviticus 15:24

uchafu wake utiririkao

"mtirirkiko wake najisi" au "damu yake itokayo kwenye mji wa mimba"

atakuwa najisi

Tazama maelezo ya sura 13:20

Leviticus 15:25

atakuwa kama alivyokuwa kwenye siku zake za hedhi

Hii humaanisha kwamba mwanamke atokwaye damu kutoka kwenye mji wake wa mimba wakati mwingine wowote badala ya ule wa hedhi yake ya kawaida, yeye bado ni najisi kama tu wakati wa hedhi yake.

Yeye ni najisi...yeyote amgusaye...atakuwa najisi

Tazama maelezo ya sura 13:20

a kila kitu akaacho juu yake kitakuwa najisi

Tazama maelezo ya sura 13:20

Leviticus 15:28

Lakini yeye

Neno "yeye" humaanisha mwanamke aliyedamuni"

ametakaswa kutoka kwenye kutokwa na damu kwake

kwa maelezo ta awali tazama 13:23. Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. "aponapo kutoka kwenye kutirirkwa kwake kwa damu"

atakuwa safi

Tazama maelezo ya sura 13:23

atajitwalia

"atachuku kwa ajili yake mwenyewe"

unajisi wa wake wa kutokwa na damu

"mtirirko wake wa damu umfanyao yeye najis"i

Leviticus 15:31

Hivi ndivyo inavyokupasa kuwatenga watu wa Israeli kutoka katika unajisi wao

Yahweh anazungumzia juu ya kuwalinda watu dhidi ya kuwa najisi kana kwamba ilikuwa ni kuwaweka watu salama mbali kutoka kwenye uchafu. "Hivi ndivyo iwapasavyo kuwakinga watu wa Israeli dhidi ya kuwa najisi"

unajisi wao

Tazama maelezo ya sura ya 13;@0

Leviticus 15:32

Hizi ndizo kanuni

"haya ndiyo mambo yapasayo kutendeka"

kumfanya najisi...humfanya najisi

Tazama maelezo ya sura 13:20

aliye katika kipindi cha hedh

"aliyedamuni" au "ananyetokwa damu kutoka kwenye mji wake wa mimba"

Leviticus 16

Leviticus 16:1

Aroni wanwanawe

Hii huwarejelea Nadabu na Abihu. Walikufa kwa sababu walileta kwa Yahweh moto ambao hakuukubali. (Tazama 10:1)

Leviticus 16:3

Hapa ndipo impasapo

"Hivi ndivyo"

kanzu yake ya ndani ya kitani

"Vazi la ndani." Hii ni nguo iliyovaliwa yapili kutoka kwenye ngozi chini ya nguo za nje.

mshipi

Kipande cha nguo ambacho hufungwa kuzunguka kiuno kifua

kilemba

kipande cha nguo ambacho hungwa kuzunguka kiuno au kifua

kutoka kwenye kusanyiko

Hiki ni kifuniko cha kichwani kilichofnywa kutoka na vitambaa vya nguo vilivyoringishwa

kutoka kwenye kusanyiko

"kutoka kwenye mkutano wa watu"

Leviticus 16:6

sadaka ya dhambi, ambayo itakuwa kwa ajili yake mwenyewe,

"sadaaka ya dhambi kwa ajili yake"

Leviticus 16:8

Mbuzi wa azazeli

"yule mbuzi anayepelekwa mbali." iAroni alitakiwa kuwa na mtu wa kumwacha huru huyo mbuzi aende nyikani.

kura imemwangukia

"yule ambaye kura imeteuliwa"

Lakini mbuzi...lazima aletwe mbele za Yahweh

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Aroni atamleta huyo mbuuzi...mbele za Yahweh akiwa hai.

Leviticus 16:11

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa kile ambacho Aroni anapaswa kufanya siku ile ya upatanisho.

amchinje huyo fahali

Aroni angeikusanya damu ya fahali kwenye bakuli ili kwamba baadaye ainyunyize juu ya kiduniko cha upatanisho. Maana kamili ya maelezo haya yaweza kuwekwa wazi.

Leviticus 16:12

chetezo

chombo kilichokuwa ajili ya moto na ubani, kilitumiwa na makuhani.

ubani...wenye harufu ya kupendeza

"ubani ulinukia vizuri." Hii ilimaanisha harufu na siyo ladha ya ubani.

Leviticus 16:14

damu ya fahali

Tazama maelezo ya sura 16:11

kuinyunyiza kwa kidole chake

Alitumia kidole chake kurushia damu

upande wa mbele wa kifuniko cha upatanisho

Aliiweka hiyo damu upande wa juu wa kifuniko. pia aliiweka upande wa pembeni mwa kifuniko uliomwelekea alipoingia eneo la patakatifu pa patakatifu

mbele za kifuniko cha upatanisho

Maana zinazo wezekani ni 1) "chini ya kifuniko cha upatanisho kenye sanduku" au 2) ardhini chini ya mbele ya kifuniko cha upatanisho."

Leviticus 16:15

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa kile ambacho Aroni anapaswa kufanya siku ile ya upatanisho.

lazima ainyunyize juu ya kifuniko cha upatanisho na mbele ya kifunuko cha upatanisho

Tazama maelezo ya sura 16:14

Naye atafanya upatanisho kwa ajili ya mahali patakatifu kwa sababu ya matendo ya unajisi ya watu wa Israeli

Tahambi za watu wa Israeli zilipanajisi patakatifu.

matendo ya unajisi...uasi...dhambi

Maneno haya kimsingi ni yale yale. Nayasisitiza kwamba watu wametenda aina zote za dhambi.

Matendo ya unajisi

Tazama amelezo ya sura 13:20

katika uwepo wa matendo yao ya unajisi.

Kile kirai "matendo yao ya unajisi" huwakilisha watu wafanyao matendo ya dhambi. : "katika uwepo wa watu wafanyao matendo ya dhambi"

Leviticus 16:17

Yapasa atoke kwenda nje na kwenda kwenye madhabahu hapo mbele za Yahweh

Hii ni madhabahu ya dhabihu iliyo ndani ya uwanda wa hema

kufanya upatanisho kwa ajili ya hiyo

Kama lilivyo eneo la hema la kukutania, madhabahu nayo ni najisi kwa sababu ya dhambi za watu.

pembe za madhabahu

Tazama maelzo ya sura 4:6

ili kuitakasa

Tazama maelezo ya sura 13:23

kuitenga kwa ajili ya Yahweh, mbali na matendo ya unajisi ya watu wa Israeli.

Madhabahu kuwa imetengwa kwa imezungumziwa kana kwamba ilikuwa imetengwa na dhambi za watu kimaumbile

matendo ya unajisi

Tazama maelezo ya sura 13:20

Leviticus 16:20

lazima atamleata huyo mbuzi aliyehai

Mbuzi hyu anaitwa wa azazeli katika 16:8

kukiri juu yak

"kukiri juu ya mbuzi"

ataweka hizo dhambi juu ya kichwa cha huyo mbuzi

Hapa matendoya Aroni yalikuwa ishara ya uhamisho wa dhambi za watu kwenda kwa mbuzi kama ishara kwamba huyo mbuzi angebeba adhabu kwa ajili ya hatia yao.

maovu...uasi...dhambi

Haya yote kimsingi yanamaanisha jambo moja. Aroni anaungama kila aina ya dhambi watu waliyoitenda.

Leviticus 16:23

na kuvua mavazi ya kitani

Haya yalikuwa mavazi maalum aliyovaa Aroni pekee alipoingi patakatifu pa patakatifu.

Yapasa aoge mwili wake kwa maji mahali patakatifu

"Mahali Pataktifu" haimaanishi kwenye hema la kukutania. Hili lilikuwa ni eneo tofauti lililotengwa kwa ajili yake kuoga humo.

kuvaa nguo zake za kawaida

Haya ni mavazi ambayo Aroni alivaa kwa ajili ya majukumu yake ya kawaida.

Leviticus 16:25

Naye yapasa kuyatekeza

"Aroni yapasa yateketeze"

Huyu mtu anayemwachia mbuzi wa azazeli huru, lazima afue nguo zake na kuoga mwili wake katika maji

Mtu huyu alikuwa najisi kwa sababu kugusana na na huyo mbuzi wa azazeli, aliyebeba dhambi ya watu.

mbuzi wa azazeli

Tazama maelezo ya sura 16:8

Leviticus 16:27

ambaye damu yake ililetwa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ambaye damu yake Aroni aliileta"

lazima wapelekwe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yapasa mtu fulani ambebe"

ngozi zao

"ngozi zao" "zao" hapa humaanibsha fahali na mbuzi

Leviticus 16:29

kwa ajili yenu

Neno "yenu" humaanisha watu wa Israeli.

katika mwezi wa saba, siku ya kumi ya mwezi,

Huu ni mwezi wa saba wa kalenda ya Kiebrania. Siku ya kumi ni karibu na mwisho wa mwezi wa septemba kwenye kalenda ya kimagharibi.

upatanisho utafanywa kwa ajili yenu

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Aroni atafanya upatanisho kwa ajili yenu"

kuwatakasa ninyi...ili muwe safi

Tazama maelezo ya sura ya 13:23

kwa ajili ya kusanyiko la watu.

"kwa ajili ya watu wote wa Israeli"

Leviticus 16:32

ambaye atapakwa mafuta na kuwekwa wakfu

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "watakayempaka mafuta na kumweka wakfu.

katika nafasi ya baba yake

Kuhani mkuu alipokufa , mmoja wa wanawe angechukua nafasi yake.

mavazi matakatifu

Hizi ni nguo maalum alizopaswa kuzivaa kuhani mkuu alipoingia mahali patakatifu pa patakatifu

kwa ajili ya kusanyiko la watu.

"kwa ajili ya watu wote wa Israeli"

Leviticus 16:34

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anamaliza kumwambia Aroni kile ambacho watu yawapasa kufanya.

Hili lilifanyika kama Yahweh alivyomwamuru Musa.

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utengaji. : "Naye Musa akafanya kama alivyoamru Yahweh" au "Naye Aroni akafanya kama Yahweh alivyomwamru Musa"

Leviticus 17

Leviticus 17:1

mbele za hema

"mbele za hema la Yahweh"

mtu huyo ni sharti akatiliwe mabali kutoka miongoni mwa watu wake

Tazama amelezo ya sura 7:19. : "mtu huyo yawezekana asiishi miongoni mwa watu wke" au yapasa mmtenge mtu huyo na watu wake"

Leviticus 17:5

kwa kuhani ziweze kutolewa kuwa sadaka

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "kwa kuhani ili kwamba aweze kuwatoa dhabihu"

Leviticus 17:7

ambazo kwazo hutenda kama makahaba

Watu ambao wamekuwa siyo waaminifu kwa Yahweh kwa kuabudu miungu ya uongo wamezungumziwa kana kwamba walikuwa akitenda kama mwanaume anayemsaliti mkewe kwa kufanya uzinzi. : "ambayo kwa ajili yake siyo waaminifu kwa Yahweh"

Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yao katika vizazi vya watu wao vyote

Tazama maelezo ya sura 3:15

Leviticus 17:8

mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake

Tazama maelezo ya sura 7:19 na ya suara 17:4

Leviticus 17:10

Nitaukaza uso wangu dhidi ya mtu huyo

Neno "uso" huwakilisha nafsi. Nahu hii humaanisha kumkataa mtu au kitu fulani. : "Nitakuwa nyume na mtu huyo" au "nitamkataa mtu huyo" au "Nitamkataa huyu mtu"

kumkatilia mbali atoke miongoni mwa watu wake

Mtu aliyeondolewa kwenye jamii yake anazungumziwa kana kwamba amekatwa kwa watu wake, kama mtu akatavyo tawi kutoka kwenye mti. : "Sitamruhusu mtu huyu aendelee kuishi miongoni mwa watu wake tena"au "Nitamtenga mtu huyo kutoka kwa watu wake"

Kwa kuwa uhai wa mnyama yeyote umo katika damu yake...ipatanishayo kwa ajili ya uhai

Hii humaanisha MUngu huitumia damu kupatanisha kwa ajili ya dhambi za watu kwa sababu damu ni uhai. Watu wasinywe damu kwa sanbabu ina kusudi hili maalum.

Leviticus 17:12

Niliwaambia

"Niliwambia" hapa humaanisha Yahweh

asiwepo miongoni mwenu impasaye kula damu

"asiwepo mingoni mwenu awezaye kula nyama pamoja na damu ndani yake"

awezaye kuliwa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ambao nilisemba wanaweza kuwala"

na kuifukia kwa udongo hiyo damu

"na kuifunika damu mavumbi"

Leviticus 17:14

uhai wa kila kiumbe umo katika damu yake

Hii humaanisha kwamba damu ndiyo ikiwezeshayo kiumbe kuishi. Maana kamili ya kauli hii yaweza kufanywa wazi. "kila kiumbe chaweza kuishi kwa sababu ya damu yake"

Yeyote ailaye ni lazima akatiliwe

Mtu aliyeondolewa kwa jamii yake anazungumziwa kana kwamba amekwisha kukatwa kutoka kwa watu wake, kama vile mtu angeweza kipande cha nguo au tawi la mti kutoka kwenye mti. : "yeyote alaye damu hataweza kuishi tena miongoni mwa watu wake" au "yeyote alaye damu sharti mmtenge na watu wake"

Leviticus 17:15

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuzungumza.

ambaye amelaruliwa na wanyama pori

Mnyama anayeuawa na wanyama pori anazungumziwa kana kwamba hao wanya pori wamchana vipande vipande huyo mnyama. Hii yaweza katika mtindo wa utendaji. : ""yule ambaye wanyamapori wamemuua"

ni mwenyeji wa kuzaliwa

"ni Mwisraeli"

naye atakuwa...Kisha ndipo atakuwa safi

Tazama maelezo ya 13:20 na 23

Hata Jioni

"mpaka macheo"

sharti yeye aichukue hatia yake

Hatia ya mtu imezungumziwa kana kwamba ilikuwa kitu ambacho mtu hukibeba. Neno "hatia" hapa huwakilisha adhabu kwa hatia hiyo. : "Hivyo anawajibika kwa hatia yake mwenyewe" au "kisha nitamwadhibu yeye kwa ajili ya dhambi yake"

Leviticus 18

Leviticus 18:1

Yahweh

Hili ni jina Mungu ambalo alimwambia Musa kwenye kicha kilichowaka moto. Mungu alisema kwamba hili ndilo lilikuwa jina lake milele.

Musa

Musa alikuwa nabii na kiongozi wa watu wa Waisraeli kwa zaidi ya miaka 40.

Alipokuwa mtoto, wazazi wake Musa, walimweka yeye kwenye kikapu cha mianzi ya Mto Nile ili kumficha kwa Farao wa Misri. Dada yake Miriamu dada yake Musa, Alimwangalia yeye huko. Maisha ya Musa yaliokolewa tu binti alipomwona na kumchukua kwenda naye Ikulu ili kumlea kama mwanae.

Mungu alimchagua Musa kuwaweka huru Waisraeli kutoka utumwani Misri na kuwaongoza kwenda katika Nchi ya Ahadi.

Baada ya kutoka kwa Waisraeli Misri na walipokuwa wangali wakizunguka jangwani, Mungu alimpa Musa mbao mbili za mawe zilioandikwa Amri Kumi juu yake.

Karibu kabisa na mwisho wa maisha yake, Musa aliiona tu Nchi ya Ahadi, lakini haingia kuishi humo kwa sababu hakumtii Mungu.

Kikundi cha watu, watu, watu wa,

Ule usemi "watu" au "vikundi vya watu" humaanisha vikundi vya watu wanaoshiriki lugha na utamaduni mmoja. Kile kirai "watu wa" mara kwa mara humaanisha kusanyanika la watu katika eneo fulani au katika tukio maalum.

Mungu anapotenga "kikundi cha watu" kwa ajili yake, humaanisha alichagua watu fulani ili wawe wake na kumtumikia yeye.

Katika nyakiti za Biblia, washirika wa kikundi cha watu kwa kawaida walikuwa na wazazi au mababu wamoja na waliishi mahali pamoja katika taifa au eneo maalum la nchi.

Kwa utegemeana na muktadha, kirai kama vile "watu wako" chaweza kumaanisaha "kikundi cha watu wako" au "famikia yako" au "jamaa zako."

Ule usemo "watu" mara kwa mara limetumika kumaanisha vikundi vyote vya watu juu ya nchi." Wakati mwingine zaidi lilimaanisha hasa kwa watu wasio Waisraeli au wasiomtumikia Yahweh. Katika tafasiri zingine za kiingereza ule msemo "mataifa" pia umetumika katika njia hii.

MAPENDAKEZO YA UFASIRI. Ule msemo "kikundi cha watu" waweza kufasiriwa kwa neno au kirai chenye kumaanisha, "kundi kubwa la kifamilia" au "ukoo" au "kikundi cha kikabila."

Kirai kama vile "watu wangu" chaweza kufasiriwa kama "jamaa zangu" au "Waisraeli wenzangu" au "familia yangu" au "watu wa kikundi changu," kutegemeana na muktadha.

Yale maelezo "nitawatawanya miongoni mwa watu" pia yaweza kufasiriwa "nitasababisha kwenda na kuishi pamoja na vikundi mbali mbali vya watu wengi" au "sababisha kutengana ninyi kwa ninyi na kwenda kuishi katika mikoa mingi tofauti ya ulimwengu.

Ule msemo "watu" waweza kufasiriwa "watu ulimwenguni" au "vikundi vya watu," kutegemeana na muktadha.

Kile kirai "watu wa" chaweza kufasiriw kama, "kila mmoja aishie katika" au "watu wa kutoka uzao wa" au "familia ya," kutegeana na ama linafuatiwa na jina la mahali au mtu.

"watu wote wa ulimwengu" yaweza kufasiriwa kama, "kila nafsi ulimwenguni" au "watu wote."

Kile kirai "watu" pia chaweza kufasiriwa kama "kikundi cha watu" au "watu fulani" au "kikundi cha watu" au "jamii ya watu" au "familia ya watu"

Israeli, Waisraeli, taifa la Israeli

Ule msemo "Israeli" ni jina ambalo Mungu alimpa Yakobo. Humaanisha, "yeye hushindana na Mungu."

Wazao wa Yakobo walikuja kujulikana kama "watu wa Israeli," "taifa la Israeli," au "Wasraeli." Taifa la Israeli

Mungu alitengeneza agano lake watu wa Israeli. Walikuwa watu wake wateule.

Taifa la Israeli liliundwa na makabila kumi na mbili.

Mara tu baada ya kufa kwa mfalme Sulemani, Isrseli iligawanyika katika falme mbili: Ufalme wa kusuni, uliitwa "Yuda" na ule ufalme wa kaskazini ukaitwa "Israeli."

Mara kwa mara ule msemo "Israeli" waweza kufasiriliwa kama, "watu wa Israeli" au "taifa la Israeli," kwa kutegemeana na muktatha.

Mungu

Kwenye Biblia Neno "Mungu" humaanisha nafsi ya milele aliyeumba ulimwengu pasipo kitu. Mungu huishi kama Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu. jina binafsi la Mungu ni "Yahweh" . Siku zote Mungu alikuwapo; alikuwapo kabla ya kabla ya kitu chochote kuwapo. Naye ataendelea kuwako milele

. Yeye ndiye Mungu wa kweli na ana mamlaka juu ya vitu vyote hulimwenguni.

. Mungu ni mwenye haki kwa ukamilifu, ni mwenye hakima pasipo na kikomo, mtakatifu, bila dhambi, mwenye haki, rehema, na upendo.

. Yeye ni Mungu atunzaye agano, ambaye hutimiza ahadi zake.

. Watu waliumbwa ili wamwambudu Mungu naye ndiye Yeye pekee imewapasa wao kumwabudu.

. Mungu lilifunua jina lake kuwa ni "Yahweh" ambalo humaanisha, " yeye ndiye" au "Mimi ndimi" au "Yule aliyopo (siku zote)"

. Pia Biblia hufundisha juu ya "miungu ya uongo" ambayoo ni sanamu zisizo na uhai ambayo watu huiabudu kimakosa.

MAPENDEKEZO YA UFASIRI

. Njia za kufasiri "Mungu zingejumuisha maneno kama "Uungu" au "Muumba" au "Mwenye Mamlaka yote"

. Njia zingine za kufasiri "Mungu" zaweza kuwa, "Muumbaji wa vyote" au "Bwana Mwenye mamlaka isiyo na mipaka" au "Mwenye Mamlaka yote milele."

Zingatia jinsi Mungu anavyotajwa katika lugha ya kieneo au kitaifa. Yawezekana kuwa tayari lipo neno kuhusu "Mungu" katika lugha inayotafsiriwa. Kama ndivyo, ni muhimu kuhakikisha kwamba neno hili linafaa kwa sifa baishi za Mungu wa kweli kama anavyoelezwa hapo juu.

Lugha nyingi huanza na herifu kubwa ya neno kwa Mungu aliye wa kweli ili kulitofautisha na neno kwa mungu wa uongo.

Njia nyingine ya kuonesha tofauti hizi ingetumika misemo miwili tofauti kwa "Mungu" na "muungu"

Kile kirai, "nitakuwa Mungu wao nao watakuwa atu wangu" pia chaweza kufasiriwa kama, "Mimi, Mungu, nitatawala juu ya watu nao wataniabudu mimi."

Misri, Mmisri

Misri ni taifa lililoko upande wa kaskazini mashariki mwa Africa, kusini magharibi mwa nchi ya Kanaani. Mmisri ni mtu anayetoka katika nchi ya Misri.

. Zamani za kale, Misri lilikuwa taifa lenye nguvu na tajiri.

. Misri ya zamani iligawanyika katika sehemu mbili, Misri ya chini (sehemu ya kaskazini mahali ambapo mto Nile ulitiririka kuelekea Baharini) na Misri ya juu (sehemu ya kusini). Katika Agano la Kale, sehamu hizi zilitajwa kama "Misri" na "Pathrosi" katika lugha ya asili.

Mara nyingi kilipokosekana chakula huko Kanaani, mababa wa Israeli walisafiri kwenda Misri ili kununua chakula kwa ajili aya familia zao.

Kwa muda wa mamia ya miaka, Waisraeli walikuwa watumwa huko Misri.

Yusufu na Mariamu waliterekia Misri pamoja na mtoto mchanga Yesu ili kumtoroka Herode Mkuu.

Maisha, ishi, kuishi, -wa mzima

Misemo hii yote humaanisha kuwa mzima kimaumbile, siyo mfu. Pia yametuka kiishara kumaanisha kuwa hai kiroho. Ifuatayo inazungumzia inavyomaanisha kuwa na "uhai wa kimwili" na "Uhai wa Kiroho"

MAPENDEKEZO YA UFASIRI

. Kwa utegemeana na muktadha, "maisha yaweza kufasiriwa kama "uwepo" au "nafsi" au "moyo" au "aishie" au "uzoefu"

. Ule msemo "ishi" waweza kufasiriwa "kaa" au "kuwepo."

Yale amelezo "mwisho wa maisha" yangeweza kufasiriwa kama, "alipokoma kuishi."

Yale maelezo "alitunza uhai wao" yangeweza kufasiriwa kama, "aliwaruhusu kuishi" au "hakuwaua wao."

Ule usemi "walihatarisha maisha yao" ungeweza kufasiriwa kama, "walijiweka wenyewe hatarini" au walifanya jambo fulani ambalo lingekuwa limishawaua wao."

Kifungu cha Biblia kinapozungumzia kuwa hai kiroho, "uhai"pia ungefasiriwa kama, "maisha ya kiroho" au "Uzima wa milele" kutegemeana na muktatha"

Wazo la "maisha ya kiroho" lingeweza kufasiriwa pia kama "Mungu anatufanya hai katika roho zetu" au "maisha mpya yatolewayo na Roho wa Mungu" au "kufanywa hai katika utu wetu wa ndani."

Kwa kutegemeana na muktatha, neno "-pa maisha" laweza pia kufasiriwa kama "sababisha kuwa hai" au -pa maisha mapya" au "sababisha kuishi milele."

Leviticus 18:4

Sheria zangu ndizo mtakazozitenda, na amri zangu ndizo mtakazozishika

Virai hivi viwili kimsingi humaanisha kitu kile kile na vinasisitiza kwamba ni sharti watu watii kila jambo ambalo Mungu amewaamru wao walitende. Msambamba huu waweza kufasiriwa kwaiti kauli moja inayowasilisha matakwa ya kutunza amri zote za Yahweh. : "Yapasa mzitii sheria na namri zote"

Ili kwamba mpate kutembea katika hizo

Kutii amri za Yahweh kumezunguziwa kana kwamba kulikuwa njia ambayo juu yake mtu hutembea. : "ili kwamba mweze kusimamia mwenendo yenu kulingana na hizo.

Leviticus 18:6

wake za baba yako

Wakati mwingine wanaume walikwa na zaidi ya mke mmoja. Mungu hakumruhusu mwana kulala na mwanamke yeyote aliyeolewa na baba yake.

Leviticus 18:9

ama ni binti ya baba yako au ni binti ya mama yako

Hii humaanisha mwanaume hawezi kulala na iwapo wa mazazi wale wale hata kama ana mama au baba tofauti.

ama aliyelelewa nyumbani mwenu au mbali nawe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ama alikulia nyumbani kwenu au mbali"

Usilale na binti ya mke wa baba yako,

Maana mbili zinazowezekana ni 1) "usilale na dada yako wa kambo au 2) "usilale na dada yako wa kunyonya." Hapa mwanaume hana baba au mama mmoja na mwanamke. walikuwa kaka na dada wazazi wao walipooana.

Leviticus 18:12

Usimkaribie kwa kusudi hilo

"Usimwendee kwa kusudi la kulala naye"

Leviticus 18:15

usilale naye

Yahweh analirudiia hili ili kuisisitiza amri hii.

Leviticus 18:17

uovu, ufisadi, upotovu

Ile misemo "uovu" na "ufisadi" yote mawili humaanisha jambo lolote linalopingana na tabia na mapenzi matakatifu ya Mungu.

Neno "uovu" linapoweza kuelezea tabia ya mtu, neno, ufisadi linaweza kuhusiana na tabia tabia ya mtu, Hata hivyo, misemo yote miwili hufanana katika maana.

Ule msemo" upotovu" humaanisha ile hali ya kuwawepo watu wafanyapo mambo maovu.

Yale matokeo ya uovu huonyeshwa wazi katika namna watu wanavyotendea vibaya wengine kwa kuua, kuiba, kulahgai, au kuwa wakatili na kutokuwa na huruma.

MAPENDEKEZO YA UFASIRI Kwa kutegemea namuktatha, ile msemo "ovu" na "fisadi" yaweza kufairiwa "baya" au"-enye dhambi" au "-siyo adilifu."

Njia nyingine za kufasiri haya zaweza kujumuisha, "siyo -ema, "isiyo nyofu" au "isiyo adilifu."

Hakikisha kwamba yale maneno au virai vinavyotumika kufasiri misemo hii ni vyenye kufaa kwenye muktadha vilivyo vya asili katika lugha lengwa.

uhai, ishi, maisha, -wa hai

Tazama maelezo ya sura 18:3

Leviticus 18:19

hedhi

Hiki ni kipindi cha majira ambapo mwanamke anapotokwa damu kutoka kwenye mji wake wa mimba.

yeye ni najisi

Tazama maelzo ya sura ya 13:20

mke wa jirai yako

"muke wa mwanaume yeyote"

Leviticus 18:21

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa watu kisichowapasa kukifanya ambacho kingewachafua wao.

Msiwatoe watoto wenu ili kuwapitisha kwenye moto

Kile kirai "kuwapitisha kwenye moto" humaanisha kuwachoma kitu kwa moto kwa dhabihu. : "Msiwachome moto wato wenu wangali hai"

msije mkalikufuru jina la Mungu wenu

"KNeno "kukufu" hapa ni kufedhehesha. Neno "jina" humwakilisha Mungu mwenyewe. : "msimfedheheshe MUngu wenu."

Leviticus 18:22

hili lingekuwa uovu

"Uovu" hapa hurejelea ukiukaji wa mfumo wa vitu vya asili kama Yahew alivyovitarajia viwe.

Leviticus 18:24

mataifa yamechafuliwa

Hii humaanisha vikundi vya watu vinavyoishi huko Kanaani. Hii inafaa kufasiriwa ili kwamba ule msemo "mataifa" uwekwe wazi kuwa ni "watu." : "watu wa mataifa walijichafua wenyewe"

Nayo nchi imenajisiwa

"Watu waliichafua nchi"

nayo nchi ikawatapika wakazi wake

Yahweh akiwawaondoa watu kwa nguvu kutoka katika kunazungumziwa kana kwamba nchi ilikuwa mtu ambaye aliwatapika watu. : "Ikiwa aliwaondowa watu kwa nguvu kutoka katika nchi, kama vile mtu atapikavyo chakula"

Leviticus 18:26

aina yoyote ya mambo haya ya machukizo

"lolote haya mambo ya kuchukiza"

haya ya machukizo

Hii iinamaanisha "mambo haya ya machukizo."

Kwa hiyo, muwe waangalifu

"Kwa hiyo basi iwenu waangalifu"

ili kwamba nchi isiwatapike nyinyi baada ya kuwa mmeinajisi, kama ilivyowatapika wale watu

Tazama maelezo ya sura 18:24. : "ili kwamba ninawaondoa kwa nguvu mtoke katika nchi...kama nilivyowaondoa kwa nguvu hao watu"

Leviticus 18:29

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anamaziliza kumwambia Musa kinachowapasa watu kunda.

watu...watakatiliwa mbali kutoka miongoni mwa watu wao

Tazama lilifasiwa katrika sura zilizotangulia.

ambazo zilitendwa hapo kabla yenu

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. :"ambayo watu waliyatenda hapa kabla yenu"

kwazo

"Kwazo" hapa hurejelea desturi zenye machukizo

Leviticus 19

Leviticus 19:1

muzishike Sabato zangu

"tunza Sabato zagu" au "heshimu siku yangu ya mapumziko"

Msizigeukie sanamu zisizo na thaman

Kule kuabudu sanamu kumezunguzungumziwa kana kwamba ilikuwa ni kugeukia kwao kimaumbile

Leviticus 19:5

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa kinachowapasa watu kukifanya

utatoa ili kupata kibali.

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. Maana zinazowezekana ni 1) Yahweh atampokea mtu atoaye hiyo dhabihu. : "yapasa uilitoe ili kwamba huenda atakupokea" au 2) Yahweh ataikubali dhabihu kutoka kwa huyo mtu. : "yakupasa kuitoa ili kwamba huenda Yahweh ataipokea dhabihu yako."

sharti iliwe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Sharti muile"

lazima kiteketezwe kwa moto

Tazama maelezo ya 19:6

Endapo kitaliwa hata kidogo

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Ikiwa utakula hata sehemu hata yake yoyote"

Hakitakubalika

Kula sadaka baada ya wakati ulioteuliwa ni kwenda kinyume na Mungu na huongeza hatia ambayo dhambi ilikuwa iifunike. Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "usiikubali hiyo kwa ulaji"

kila akilaye ni lazima atachukua hatia yake

Ile hati ya mtu imezungumziwa kana kwamba illikuwa kitu chenye maumbile ambacho mtu hukibeba. Neno "hatia" hapa huwakilisha ile adhabu kwa hatia hiyo. : Kila mmoja...anawajika kwa hatia yake mwenyewe" au Yahweh atamwadhibu kila mmoja...kutokana na dhambi zake mwenyewe

Mtu huyo sharti atakatiliwa mbali na watu wake

Tazama lilivyofasiriwa katika 7:19 : "inawezekana mtu huyo asiendelee kuishi kuishi miongoni mwa watu wake" au "ni lazima mmtenge mtu huyo na wa watu wake"

Leviticus 19:9

Unapovuna mavuno ya ardhi yako, usivune hata pembezo mwa shamba lako kabisa

"Unapokusanya mazao yako, usiyakusanye yote hata mipakani mwa mashamba yako"

wala hutakusanya mabaki ya mavuno yako yote

Hii hurejelea ile desturi ya kurudia kuvuna shambani kama kipindi cha pili cha kukusanya mazao yaliyobaki baada ya kipindi cha kwanza. Maana kamili ya maelezo haya yaweza kuwekwa wazi. : "na usirudi nyuma uvunapo shambani na kuokota masalio yote uliyoyaachia nyuma"

Leviticus 19:11

Usiape kwa jina langu kwa uongo

"Usilitumia jina lwangu kuapa juu ya jambo fulani ambalo siyo la kweli.

Leviticus 19:13

Usimgandamize jirani yako wala kumwibia

"Jirani" hapa humaanisha "yeyote"Maana ya hili yaweza kuwekwa wazi. : "usimuumize wala kumwibia yeyote"

Usishikilie malipo ya kibarua usiku kucha hata asubuhi

Yahweh anamwamru mwajiri kumlipa kwa haraka mtumshi wake mara kazi yake inapokamilika siku hiyo hiyo. Maana kamili ya tamko hili yaweza kufanywa wazi.

Leviticus 19:15

Usisababishe hukumu ikawa ya uongo

Hii hasi ya maradufu imetumika kusisitiza. Inaweza kuelezwa katika nji chanya. : "Hukumu kwa haki siku zote"

Usionyeshe upendeleo kwa mtu fulani eti kwa kuwa tu yeye ni masikini na usionyeshe upendeleo kwa mtu fulani eti kwa kuwa tu yeye ni mtu muhimu

Yale maneno "masikini" na "muhimu" ni mambo mawili yenye kukithiri, ambayo kwa pamoja humaanisha "yeyote." : "Haikupasi kuonyesha upendeleo kwa yeyote kwa msingi wa kiasi cha wingi wa fedha walizo nazo.

amua juu ya jirani yako kwa haki

""mhukumu kila mmoja kwa kulingana na haki"

Usiende huku na huko ukisema habari za uchochezi

"Usiende huku na huko kwa watu wengine huku ukisengenya"

Leviticus 19:17

Usimchukie ndugu yako moyoni mwako

Kule kumchukia ndugu yako kwa kuendelea kumezungumziwa kana kwamba kulikuwa kumchukia mtu ndani ya moyo. : "Ussimchukie ndugu yako wa kuendelea"

Mkemee jirani yako kwa heshima

"Yapasa umrekebishe anayetenda dhambi"

Leviticus 19:19

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa yawapasayo watu kutenda.

vazi lililofumwa kwa kutumia nyuzi za rangi mbili tofauti zilizochanganywa pamoja

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "vazi ambalo mwingine alilitengeneza kutokana na nyuzi za aina mbili"

Leviticus 19:20

aliyeposwa na mume mwingine

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "liyeahidiwa kuolewa na mwanamume mwingine"

lakini ambaye hajakombolewa au hajaachwa huru

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ambaye mume wake mtarajiwa hajamkomboa au kumpa uhuru"

lazima waadhibiwe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "niyapasa kumwadhibu huyo msichana mtumwa na hyuo mwanaume aliyelala naye"

Hawatauawa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Haiwapasi kuwaua"

mtu huyo alete sadaka yake ya hatia kwenye ingilio la hema la kukutania—kondoo dume iwe sadaka ya hatia

Huyo mwanaume atalazimika kuleta kondoo dume kwenye ingili la hema ya kukutania kuwa sadaka ya hatia kwa Yahweh"

Nayo dhambi iliyotendwa itasamehewa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Naye Yahweh ataisameheme dhambi aliyoitenda"

Leviticus 19:23

Taarifa kwa Ujulma

Yahe anaendelea kumwambia Musa yawapasayo watu kutenda.

kisha mtayahesabu matunda yatakayozaliwa kuwa yamekatazwa kuliwa. Halitaliwa

Yahweh analirudia katazo ili kulikazia na kuweka wazi kwamba ni lazima kwa miaka mitatu ya kwanza ya mti kuzaa matunda. Ni lazima kuwe na kipindi maalum kwa miti kuachwa peke yake. : "nawe hutakula matunda ya miti kwa miaka mitatu ya kwanza"

Tunda litakatazwa kwako

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Nimelikataza tunda kwako"

Nalo alitaliwa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Sharti usilile"

Leviticus 19:26

damu

Msemo "damu" humaanisha kimiminika chekundu kinachotoka kwenye ngozi ya mtu panapokuwa na jeraha au kovu. Damu huleta virutubisho vitoavyo uhai kwa mwili mzima wa mtu.

  • Damu hutoa ishara ya uhai na

    inapomwagwa au kutolewa nje, hutoa ishara ya kupoteza maisha, au kifo

  • Watu waliotoa dhabihu kwa Mungu, waliua

    mnyama na waliimimina damu yake juu ya madhabahu. Hili lilitoa ishara ya dhabihu ya uhai wa mnyama kulipa dhambi za mtu.

  • Kwa kupitia kifo chake msabani, kiishara

    damu ya Yesu iliwasafisha watu kutoka katika dhambi zao na hulipa ile adhabu wanayostari kwa ajili ya dhambi hizo dhambi zao

  • Yale maelezo "nyama na damu" humaanisha

    wanadamu

  • Yale maelezo "mwili na damu yako

    mwenyewe" humaanisha watu wanaohusiana kizazi

MAELEZO YA UFASIRI

  • Msemo huu sharti ufasiriwe na msemo

    unaotumika kwa damu katika lugha lengwa

  • Yale maelezo "mwili na damu" yangeliweza

    kufasiriwa kama "watu" au viumbe vyenye uhai."

  • Kulinga na muktatha, yale maelezo "nyama

    na damua yangu mwenyewe "waweza kufasiriwa kama "familia yangu mwenyewe" au "jamaa yangu mwenyewe" au watu wangu mwenyewe."

  • Endapo kutakuwa na maelezo yoyote katika

    lugha lengwa yanayotumika pamoja na maana hii, yangeweza kufasiri "mwili na damu"

roho, -a kiroho

Msemo roho hulenga sehemu ya watu isiyo na maumbile isiyoweza kuonekana. Mtu anapokufa, roho yake huuacha mwili wake. Pia "roho" yaweza kumaanisha tabia au hali ya kujisikia.

  • Ule msemo "roho" waweza kumaanisha

    kiumbe kisicho na mwili unaoonekana, hasa roho ovu.

  • Roho ya mtu ni sehemu yake inayoweza

    kumjua Mungu na kuamini katika Yeye.

  • Kwa ujumla msemo "-a kiroho" hukielezea

    chochote katika ulimwengu usio na maumbile

  • Kwenye Biblia, hasa hulenga chochote kile

    kinachohusiana na Mungu, moja kwa moja kwa Roho Mtakatifu.

  • Kwa mfano, "chakula cha kiroho" huhusiana

    na mafundisho ya Mungu yatoayo lishe kwa roho ya mtu, "Ile "hekima ya kiroho" humaanisha ufahamu na tabia adilifu inayotokana na uweza wa Roho Mtakatifu.

  • Mungu ni Roho naye aliumba viumbe roho

    wengine wasio na miili ya kuonekana.

  • Malaika ni viumbe roho, pamoja na wale

    walioasi dhidi ya Mungu na wakawa roho waovu.

  • Ule msemo "roho ya" pia waweza

    kumaanisha "kuwa na tabia bainishi za," kama vile katika, "roho ya hekima" au "katika roho ya Eliya."

  • Mifano ya "roho" kama nia au hisia

    ungejumuisha "roho ya woga" au "roho ya wivu"

MAPENDEKEZO YA UFASIRI

  • Kwa kutegeana na muktadha, baadhi ya njia

    za kufasiri "roho" zinaweza kuhusisha, "kiumbe kisicho na maumbile" au "sehemu za ndani" au "utu wa ndani."

  • Katika mazingira mengine, ule msemo "roho"

    waweza kufasiriwa kama "roho ovu" au "kiumbe roho ovu"

  • Wakati mwingine ule musemo "roho"

    umetumika kuelezea hisia ya mtu aka vile, "roho yangu ilihuzunishwa katika utu wangu wa ndani." Hii pia yaweza kufasiriwa kama, "nilijisikia kuhuzunishwa rohoni mwangu" au "nilisikia kuhuzunishwa mno."

  • Kile kirai roho ya" chaweza kufasiriwa kama,

    "mwenendo wa, au ushawishi wa," au "nia ya" au fikira"

uweza, weuzo

Ule msemo "uweza" humaanisha uwezo wa kufanya mambo au kusababisha mambo yatokee, mara kwa mara kwa kutumia nguvu kubwa. "Uwezo" humaanisha watu au roho zenye uwezo wa kusababisha mambo kutokea.

  • Ule "uweza" wa Mungu hurejelea uwezon

    wa Mungu wa kufanya mambo yatokee, hasa mambo yasiyowezekana kwa watu kuyatenda.

  • Mungu anauweza kamili juu ya kila kitu

    ambacho amekiumba

  • ungu huwapa watu wake uwezo wa

    kufanya kile atakacho, ili kwamba wanapoponya watu au kutenda miujiza, wawe wanafanya hivi kwa uweza wa Mungu.

MAPENDEKEZO YA UFASIRI

  • Kwa kutegemeana na muktadha, ule

    msemo "uweza" pia wawweza kufasiriwa kama "uwezo" au "nguvu" au "bidii" au "uwezo wa kutenda miujiza au kudhibiti."

  • Njia zinazowezekana kufasiri msemo

    "uweza" yaweza kuhusisha "wenye uhai walio na uwezo mkubwa" au roho zenye kutawala" au "wale wanaotawala wengine"

  • Yale maelezo kama vile "utuokoe kutoka

    katika nguvu za adui zetu" waweza kufasiriwa kama, "utuokoe kutokana na kugandamizwa na adui zetu" au "utuokoe kutoka katika kutawaliwa na adui zetu." Katika hali hii, "uweza" una maana ya kutumia nguvu za mwingine kudhibiti na kugandamiza wangine.

Leviticus 19:29

Usimwaibishe binti yako kwa kumfanya kahaba, la sivyo taifa litaangukia kwenye ukahaba na nchi itajawa na uovu

Yale maneno "taifa" na "nchi" huwakilisha watu wakaao humo. Watu wengi wanaotenda ukahaba na wale wengine wanaotenda matendo ya uovu wamezungumziwa kana kwamba wameangukia au wamejawa na mambo hayo. : "Watu wataanza kufanya ukahaba na mambo mengi maovu"

Leviticus 19:31

wafu au roho wachafu

Maana zinazowezekana ni 1) wale "waf" ana "roho" ni vitu viwili tofauti 2)kwamba huku ni kujirudiarudia kunakomaanisha "roho za watu waliokufa"

msiwatafute, la sivyo watawanajisi ninyi

"Msiwatafute hao watu. kama mtafanya hivyo, watawachauweni nyinyi"

Leviticus 19:32

Ni lazima usimame

Kusimama mbele za ya mtu mwingine ni ishara ya kuheshimu.

mtu mwenye mv

mtu mwenye mvi- Hii humrejelea mtu ambaye nywele zake zimekuwa nyeupe kutokana na umri, au mtu mzee."

Leviticus 19:33

Mgeni, -a kigeni, mpitaji

Ule msemo "mgeni" humrejelea mtu anayeishi katika taifa lisilo lake mwenyewe. Jina lingine la mgeni ni "mpitaji"

Katika Agano la Kale, musemo huu hasa humlenga yeyote anayetoka katika kikundi cha watu walio tofauti ya watu aliokuwa akiishi miongoni mwao.

Mgeni pia ni mtu ambaye lugha na utamaduni wake ni tofauti na ule wa kwako

Mathalani, Naomi na familia walipohamia Moabu, walikuwa wageni huko. Naomi na binti mkwe wake Ruthu walipohamia baadaye Israeli, Ruthu aliitwa :"mgeni" huko kwa sababu kwa asili hakutokea Israelli.

Mtume Paulo anawaambi Waefeso kwamba kabla hawajamjua Kristo, walikuwa "wageni" kwa Agano la Mungu.

Wakati mwingine "mgeni" hutafriwa kama "mpitaji," lakini, haliwezi kumlenga tu mtu fulani asiyejulikana au asiyefahamika.

Mpende, penda .

Kumpenda mtu mwingine ni kumjali mtu huyo na kufanya mambo yatakayomnufaisha yeye. Kuna maana mbali mbali za "upendo" ambazo baadhi ya lugha zinaweza kuuelza kwa kutumia maneno tofauti: 1. Upendo unaotoka kwa Mungu wenyewe hulenga juu mema kwa ajili ya wengine, hata kama haujinufashi wenyewe. Iana hii ya upendo hujali wengine, haijalishi wanafanya nini. Mungu mwenyewe ni pendo na ndiye asili ya upendo wa kweli.

. Yesu alionyesha aina hii ya upendo kwa kujitoa dhabihu uhai wake ili kutokoa sisi kutoka dhambini na kifoni. Yeye aliwafundisha pia wanafunzi wake kuwapenda wengine kwa kujitoa dhabihu.

. Watu wanapowapenda wengine kwa aina hii ya upendo, huhusisha matendo yanaoonyesha kwamba mtu mwingine anafikiri juu ya kitakachosababisha mtu mwingi kufanikiwa. Upendo wa aina hii hasa huhusisha kuwasamehe wengine.

. Katika toleo la ULB, neno "upendo" humaanisha upendo wa kujito dhabihu, isipokuwa maelezo yanapoashiria kuleta maana nyingine

  1. Neno lingine katika Agano Jipya humaanisha upendo wa ndugu au upendo wa kirafiki au wa mmoja wa wanafamilia.

. Msemo huu hulenga upendo wa kibinadamu baina ya marafiki au ndugu.

. Linaweza kutumiwa pia katika mazingira kama vile, "wanapenda kukaa kwenye viti vya mbele katika karamu." Hii inamaanisha kwamba "wanapenda sana" au wanatamani sana kufanya hivyo.

  1. Neno "upendo" pia laweza kumaanisha mapenzi baina ya mwanaumme na mwanamke. 4. Katika maelezo ya kitamathali , "Yakobo nimempenda, lakini Esau nimemchukia," ule msemo "nimempenda" humaanisha Mungu kumchagua Yakobo kuwa katika uhusiano naye wa kimaagano. Hili pia laweza kufasiriwa kama "aliyechaguliwa." Ingawaje Esau pia alibarikiwa na Mungu, hakupewa upendeleo wa kuwa katika agano. Ule msemo "nimemchukia" hapa umetumka kitamathali kumaanisha "aliyekataliwa" au "asiyechaguliwa."

MAPENDEKEZO YA UFASIRI . Isipokuwa imeashiria vinginevyo kwenye maelezo ya kiufasirineno "upendo katka kwenye toleo la ULB humaanisha aina ya upendo wa kujitoa dhabihu ambao hutoka kwa Mungu

. Baadhi ya lugha zaweza kuwa na neno maalum kwa upendo usio wa kibinafsi waenye kujitoa dhabihu alionao Mungu. Njia za kuufasiri upendo huuzaweza kuwa pamoja na, "ungalizi wa kujitolea kwa uaminifu" au "jali kwa bila uchoyo" au "upendo kutoka kwa Mungu." Hakikisha kwamba neno linalotumika kufasiri upendo wa Mungu linawez kujumuisha kutupilia mbali masilahi ya mtu ili kunufaisha wengine na kupenda watu bila kujali wanachofanya

. Wakati mwingine neno "upendo" la Kiingereza huelezea uangalizi wa ndani walionao watu kwa ajili ya marafiki na wanafamilia. Baadhi ya lugha zingeweza kulifasiri neno au kirai hiki

. Baadhi ya lugha zinaweza kuwa na

Leviticus 19:35

usitumie vipimo vya udanganyifu

Hii hukataza desturi ya utuumiaji wa makusudi wa zana zinzosababisha usomaji usio sahihi wakati wa kupima vitu.

Efa

Hiki kilikuwa kipimo cha nafaka.

hini

Hiki kilikuwa kipimo kwa ajili ya vimiminika

Sharti uyatii...na kuyatenda

Virai hivi humaanisha kitu kile kile na husisitiza amri ya kutii.

Leviticus 20

Leviticus 20:1

atakayemtoa mtoto wake yeyote kwa Moleki

Wale waliomwabudu Moleki waliwatoa dhabihu watoto wao kwake kwa njia ya moto. Maana kamili yaweza kuwekwa wazi. : "auaye watoto wake kama sadaka kwa Moleki"

hakika atauawa. Ni lazima watu wa nchi wamponde kwa maw

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Watu katika nchi watamponda kwa mawe mpaka kufa

Leviticus 20:3

Pia nitaukaza uso wangu dhidi ya mtu huyo

KIle kirai "kaza uso wangu dhidi" ni nahau inayomaanisha "kumkata." : "Pia Nitamkataa" au "kumpinga vikali'

amemtoa mtoto wake

"amemtoa dhabihu mtoto wake"

ili kupatia unajisi mahali pangu patakatifu na kulinajisi jina langu takatifu

"na kwa kufanya hivyo, ampachafua mahali pangu patakatifu na kulinajisi jina langu takatifu.

najisi jina langu takatifu

Jina la Mungu humwakilisha Mungu na heshima yake. : "dunisha heshima yangu" au "kiunivunjia heshima mimi"

watayafumba macho yao kwa

Kile kirai "kufumba macho yao" huashiria "hawawezi kuona" na huwakilisha kutokuwa na uwezo wa kuelewa kwao. : "kutojali" au "puuzia"

ajifanyaye kahaba ili kufanya umalaya na Molek

Kirai hiki huwafananisha na kahaba wale wasiokuwa waaminifu kwa Yahweh. ; "yeye asiyekuwa mwaminifu kwa Yahweh"

Leviticus 20:6

ili kufanya ukahaba na

Kirai hiki huwalinganisha na kahaba wale watu wasiowaaminifu. : "kwa kufanya hivyo, wanatafuta ushauri kwa roho badala ya kuutafuta kwangu

kaza uso wangu dhidi

Tazama maelezo ya sura20:3

Leviticus 20:8

Maelezo kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa yawapasayao watu kutenda.

Mtazitunza amari zangu na kuzifuta

Yale maneno "tunza" na "fuata" kimsingi humaanisha kitu kimoja. Yametumika pamoja ili kusisitiza kwamba ni lazima watu wamtii Mungu.

hakika mtu huyo atauawa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. :"Yapasa kuua hakika"

Leviticus 20:10

Mwanaume yeyote afanyaye uzinzi na mke wa mwanaume mwingine, yaani, yeyote anayezini na mke wa jirani yake

Maana kamili sentensi hii yaweza kuwekwa wazi. : "Yule mwanaume aziniye na mke wa mtu mwingi"

lazima wote wawili wauawe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "sharti mtawaua wote wawili"

anayelala na mke wa baba yake ili kukutana naye kimwili

Hii ni ni njia ya upole ya kusema kwamba anafanya ngono na mke wa baba yake. Kuna baadhi ya lugha hutumi virai vya moja kwa moja kama vile "kufanya ngono na mke wa baba yake."

Wametenda upotovu

Hapa Mungu anamwita mwanawume anayelala na mke wa mwanae "potovu" , kuw ni dhambi mbaya sana. Tanzama katika sura 18:22 lilivyotafasiriwa ne "uovu"

Leviticus 20:13

mwanaume analala na

Tazama ililivyofasiriwa katika 20:11-12

kama alalavyo na mwanamke

Namana anavyomtendea mwanaume ndivyo angemtendea mwanamke. : "ni kama vile tu angelifanya na mwamke"

jambo lililo ovu.

"jambo la aibu" au "jambo la kuchukiza"

Hakika watauawa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yawapasa kuwaua hakika"

mwanaume huyo na manamke huyo

Tazama maelezo ya sura 20:12

Leviticus 20:15

hakika atauawa

Tazama maelezo ya sura 20:12

ni lazima mmuuwe mwanamke huyo pamoja na mnyama. Kwa hakika ni lazima wauawe

VIshazi vyote viwili humaanisha kitu kimoja. Vina sisitiza kwamba mwanamke an mnyama sharti wauawe.

Kwa hakika ni lazima wauawe

Tazama maelezoya sura 20:12

Leviticus 20:17

mwanaume analala na

Tazama maelezo hapo juu

ama ni binti ya baba yake au binti ya mama yake

Tazama katika sura zilizotangulia

Ni lazima wakatiliwe mbali watoke

Tazama maelezo ya sura 7:19

Ni lazima aibebe hatia yake

Kirai hiki humaanisha kwamba mtu anawajibika kwa thambi yale. : "Yeye anawajibika kwa dhambi yake" au "Ywawapasa kumwadhibu yeye"

kipindi cha hedhi

wakati ambapo mwanamke anatokwa damu kutoka katika tumbo lake la uzazi

atakuwa amefunua mtiririko wa damu yake, chanzo cha damu yake.

Kirai hiki kinafananisha kule kufanya ngono na mwanamke wakati akiwa kwenye kipindi chake hedhi kuwa ni sawasawa na kufunua kitu mambacho kilipaswa kubakia kimefichwa. Ule uhalisia kwamba hili liliikuwa ni jambo la aibu kukifanya linaweza kuwekwa wazi. : "amefanya jambo la aibu kwa kufunua kmtirirrko wake wa damu"

Ni lizima wote wawili wakatiliwe mbali

Yaweza kuwekwa wazi kwanini hili yapasa litendeke. : "kwa sababu wamefanya jambo hili la aibu, ni lazima wote wawili, mwanaume na mwanamke wakatiliwe mbali"

Leviticus 20:19

alalaye na

Tazama lilivyofasiriwa hapo juu

Ni lazima utabeba hatia yako mwenyewe

Tazama lilivyofasiriwa hapo juu

nitaondolea mbali mali yoyote amabayo watoto wao wangerithi kutoka kwa wazazi wao

Matleo mengi ya Biblia hulifasiri hili kama "watakufa bila kuzaa watoto."

Leviticus 20:22

ile nchi ambayo ninawaleta kuishi isiwatapike nyinyi

Tazama maelezo ya sura ya 18:24

Msienende katika

Kufanya matendo ya waabudu sanamu kumezungumziwa kana kwama ni kutembea katika njia zao. : "haiwapsi kufuata"

nitayafukuza

"ondoa"

Leviticus 20:24

nchi itiririkayo amaziwa na asal

Kile kirai itirirkayo maziwa na asali" humaanisha "iliyotajiri na yenye mazo yenye chakula cha kutosha kwa kila mmoja." : "nchi iliyonzuri kwa mifugo na kilimo" au "nchi yenye mazao"

Leviticus 20:26

nimewatenga nyinyi

"Nimewatofautisha nynyi" au "Nimewaweka kando"

Leviticus 20:27

anayeongea

Ajaribuye kuwasiliana na"

hakika atauawa

Angalia maelezo yaliyotolewa kwenye misitari mingine kwanye sura zilizotanguli.

Leviticus 21

Leviticus 21:1

Jitia unajisi mweneyewe

Tazama maelezo ta sura 13:20

miongoni mwa watu wake

"miongoni mwa Waisraeli"

bikira

Hii yaweza pia kufasiriwa mwanamke kijana"

Leviticus 21:4

pembe

"ncha"au "sehemu yoyote"

Watakuwa watakatifu

"sharti watengwe"

hawataliaibisha jina la Mungu wao

Neno "jina" limetumika kuwakilisha tabia ya Yahweh. : "wasije wakalitia aibu heshima ya Mungu" au wasije wakamfedhehesha Mungu wao"

Leviticus 21:7

Hawataoa

"Makuhani hawataoa"

kwa sababu wametengwa

"kwa sababu wamewekwa kando" (UDB)

Utamtenga

"nyinyi watu itawapasa kuwatendea makuhani kama watakatifu"

kwa sababu yeye ndiye anayetoa mkate kwa Mungu wako

"Mkate" huwakilisha chakula kwa ujumla. Yahweh huwa hali hasa matoleo haya. Yahweh huwa hali chakula isipokuwa wakuhani ndiyo walikula chakula hicho.

Ni lazima ateketezwe kwa moto

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Ni sharti mmcho moto hata kufa"

Leviticus 21:10

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia kile ambachi makuhani kinachowapasa kufanya.

Mafuta ya upako

Hii ni kumbukumbu kwa mafuta ya upako yaliyotumika kwenye ibada ya ya kumweka wakfu kuhani mkuu mpya. Maana kamili ya tamko hili yaweza kufanywa wazi.

ambaye mafuta ya upako yamekwisha kumiminwa kichwani pake, na ambaye amekwisha kuwekwa wakfu

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "amabye juu ya kichwa chake walimimina mafuta ya upako na kumweka wakfu"

kamwe hataziacha wazi nywele zake wala hatazirarua nguo zake

Kuacha nywele wazi na kurarua nguo zilikuwa ni ishara ya kuomboleza. Maana kamili ya tamko hili yaweza kufanywa wazi.

hataondoka eneo takatifu la hema la kukutania

Hii haminishi kwamba kuhani mkuu asingeweza kuondoka . Mungu hakumruhusukuondoka ili kuzunka kwa ajili ya mtu mwingine aliyekufa'

Leviticus 21:13

kutoka mipoongoni mwa watu wake

"kutoka miopngoni mwa kabila lake mwenyewe, kabila la Lawi"

asiwatia unajisi watoto wake miongoni mwa watu wake

Kwa kuoa mwanake asiyemtkatifu au asiye na hofu ya Mungu, kuhani angeweza kuwa na watoto wasiofaa kuwa makuhani. : "ili kwamba asiwe na watoto wasiostahili kwa njia ya kuoa mwanamke asiyemcha Mungu.

Leviticus 21:16

asisogee kutoa chakula kwa Mungu wake

Ile maana kamili ya kauli huii inaweza kufanywa wazi. : "impasi kuja mbele ili kuteketeza sadaka ya kuteketeswa ya chakula cha Mungu juu ya madhabahu.

Leviticus 21:18

asimkaribie Yahweh

Ilipasa kuhani awe na viwango maalum vya kimaumbile ili kumkaribia Yahweh. Hii haimaanishi kwamba kasoro za kimaumbile yalikuwa ni matokeo ya kutokuwa mwadilifu au kwamba watu alio na kasoro za kimaumbile hawana uwezo wa kumkaribia Yahweh.

aliyeharibiwa uso au kupungukiwa na viungo mwilini,

"ambaye mwili au uso wake umeharibiwa"

kutoa mkate wa Mungu wake

"Mkate" hapa huwakilisha chakula kwa ujumla. : "kufanya matoleo ya chakula juu ya madhabahu ya Mungu"

Leviticus 21:22

Anaweza

"Anayeweza" hapa ni yule kuhani aliye na kasoro za kimwili.

Kula chakula cha Mungu wake

"kula matoleo ya chakula ya Mungu wake." sehemu ya dhabihu ilikuwa ya makuhani na ingeweza kuliwa.

Wanawe

"Wana wa Aroni"

Leviticus 22

Leviticus 22:1

waambie wajiepushe na vitu vitakatifu

"waambie wakati wanaotakiwa kujiepusha na vitu vitakatifu." Yahweh anataka kuelezea mazingira ambayo kuhani huwa najisi na haruhusiwi kugusa vitu vitakatifu.

katika vizazi vyenu

"tangu sasa na kuendelea"

wakati akiwa najisi

Tazama maelezo ya sura 13:20

sharti mtu huyo akatiliwe mbali atoke mbele zangu

Yule kuhani asiyeweza tena kumtumika Yahweh amezungumziwa kana kwamba mtu huyo amekatwa kutoka mbele za Yahweh, kama mtu angekata kipande cha nguo au tawi mti kutoka kwenye mti. Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. "Mtu huyo hataweza kamwe kutumika kama kuhani"

Leviticus 22:4

ungonjwa wa ngozi wa kuambukiza

ugonjwa ujuu ya ngozi unaosambaa kwa urahisi kutoka mtu mmoja kwenda kwa mwingine

kutoka mwilini mwake

Tazama maellezo ya sura 15:1

mpaka atakapotakasika

Tama maelezo ya sura ya 13:23

yeyote agusaye kitu chochote kilichonajisi

Tazama maelzo ya sura ya 13:20"

wa njia ya kugusa maiti,

"kwa kugusa mwili wa mfu"

dhabihu iliyofanywa kwa Yahweh

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wautendaji. : "dhabihu ambayo mtu mwingine ameitoa kwa Yahweh"

au yeyote agusaye mnyama atambaaye atakayemtia yeye unajisi, au mtu yeyote atakayemfanya nyeye kuwa ajisi

Hii yaeza kfanywa wazi. : "au yeyote aliyenajisi kutokana na kugusa manyama ataambaye au kutokana na kugusa mtu aliyenajisi"

yeyote agusaye kitu chochote kisichosafi atakuwa najisi

Hii yaweza kufanywa wazi. : "au yeyote aliyenajisi kutokana na kugusa mnyama aliye mlemavu au kutokana na kugusa mtu aliye najisi"

hata jioni

"mpaka machweo"

kuhani ... atakuwa najisi

Tazama maezo ya sura ya 13:23

Leviticus 22:7

ndipo atakuwa safi

Tazama maelezo ya sura 13:23

uliookotwa au mnyama aliyeraruliwa na wanyama pori

Hii aweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ambaye mtu mwingine amemwokota akiwa amekufa au yule ambaye mnyama pori kamrarua"

Leviticus 22:10

Maelezo kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa yawapasyo Aroni na wanawe kutenda.

Leviticus 22:12

mchango wa matoleo matakatifu

Neno "mchango" laweza kufasiriwa kirai che kitenzi. : "matole matakatifu ambayo watu wamechangia"

Leviticus 22:14

naye atamlipa kuahani kwa ajili ya hicho; itampasa kuongeza moja ya tano juu yake

moja ya tano juu yake- maana zinazowe kuwa ni 1) kwamba mtu alipaswa kureje chakula kilicholiwa pamoja na chakula cha aina ile ile au 2) kwamba mtu huyo alipwa kulipa fedha kwa kuhani kawa jili ya chakula alikila yeye.

moja ya tano juu ya tano

moja ya tano juu yake- Hii ni sehemu moja kutoka kwenye sehemu matano zilizosawa.

kutoheshimu vitu vitakatifu

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yawapasa kukuvitendea kwa heshima hivyo vitu vitakatifu"

ambavyo vimeinuliwa juu na kuletwa

Kile kirai "vimeinuwa juu" hurejelea ile ishara ya heshima ninayowakilisha utoaji wa kitu fulani kwa Yahweh. Kimsingi humaanisha kitu kile kile kama "kilichotolewa." : "kile walichokitoa"

wakajisababishia wenyewe kuchukua dhambi amabyo ingewafanya kuwa na hatia

Dhambi imezungumziwa kana kwamba kilikuwa chombo ambacho watu wanaweza kukibeba. Maana za weza kuwa 1)Wangeweza kuwajibika kwa dhambi na kuwa na hatia. : "Wangekuwa na hatia kwa ajili ya dhambi waliyoitenda" au 2)neno "dhambi" kibadala cha cha adhabu kwa ajili ya dhambi waliyoitenda. : "Wangepokea adhabu kwa sababu ni wenye hatia"

Leviticus 22:17

mgeni

"mpitaji"

ikubalike,

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa kiutendaji.: "iwapo Yahweh ataikubali" au "iwapo, Mimi, Yahweh, nitaikubali"

Leviticus 22:20

ili ikubalike

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "kwa Mimi kuikubali" au "kwa Yahweh kuikubali"

Leviticus 22:22

waliojeruhiwa, wala waliotiwa kilema

Maneno haya humaanisha kasoro zilizosababishwa na ajali.

wenye upele, vidonda vitokavyo usaha, wala wenye vigaga

Haya humaanisha aina za magonjwa ya ngozi.

haitapokelewa.

"Yahweh ataikubali"

mlemavu au aliyedumaa

Maneno haya yanamaanisha kasoro ambazo mnyama anazo tangu kuzaliwa

Leviticus 22:24

Usilete mkate wa Mungu wako

"Kate" hapa huwakilisha chakula kwa ujumla. Mungu hakula dhabihu hasa. Makuhani wangetoa dhabihu juu ya madhabahu ya Mungu, na wangekula sehemu ya nyama. : "hataleta mnyama kuwa matoleo ya chakula kwa Mungu wenu"

Kutoka mkononi mwa mgeni

Neno "mkono" huwakilisha mtu mzima. Inaonyeshwa kwamba Waisraeli wasingeweza kutumia wanyama kama dhabihu iwapo wangewanunua kutokwa wageni ambao walihasi wanyama wao wakifanya wasikubalikekwa Mungu. : "ambaye mgeni amewapa , kwa sababu wao huhasi wanyamaa wao"

hawatapokelewa kabisa kwa ajili yako

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Yahweh hatawapokea kutoka kwenu"

Leviticus 22:26

anaweza kupokelewa

"unaweza kuikubali"

iliyofanywa kwa moto

"kwa ajili ya sadaka ya kuteketeza"

Leviticus 22:28

Ni lazima iliwe

"Ni lazima uile"

iyo hiyo inayotolewa

"uliyoitoa dhabiihu"

Leviticus 22:31

kuzishika amri zangu na kuzifuata

Yale maneno "Shika"na "fuata" humaanisha kitu kilekile. Nayo husisitiza kwamba ni lazima watu watii ammri za Mungu, : "tii amri zangu"

2Msiliabishe jina langu takatifu

Neno "jina" hapa humwakilisha Yahweh mwenyewe na sifa zake njema. : "msiniabishes mimi Au "msiiabishe sifa yangu njema"

Ni lazima nitambuliwe kuwa ni mtakatifu na watu wa Israeli

: "Watu wa Israeli wanitambue kwamba mimi ni mtakattifu"

Leviticus 23

Leviticus 23:1

sikukuu zilizoamriwa kwa ajili ya Yahweh

Hizi ndizo zilikuwa sikuu ambazo Bwana aliamru majira yake. Watu walikuwa wamwabudu yeye kwenye sikukuu hizi. : "Sikukuunkwa ajili ya Yahweh" au sikukuu za Yahweh"

Leviticus 23:3

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa yawapayo watu kutenda katika nyakati za ssiku maalum.

siku ya saba ni Sabato ya kupumzika kabisa

hili ni jambo ambalo watu yawapasa kulifanya kuwa mazoea yao. Kila baada ya siku sita katika watakazofaanya kazi, nilazima wapumzike katika siku ya saba.

kusaniko takatifu

Yale makwa ambayo watu walikusanyika kumwabudu Mungu katika siku hiyo yamezungumziwa kana kwamba siku hiyo ilikuwa ni kusanyiko. : "siku taktifu, ambayo yawapasa kukusanyika kuniabudu mimi"

Leviticus 23:4

nyakati zilioamriwa

"katika nyakati zake mwafaka"

mwenzi wa kwanza, siku ya kumi na nne ya mwezi ... Siku ya kumi na tano ya mwezi ule ule

Mwezi wa kwanza katika kalenda ya Kiebrania huitia alama siku Yahweh alipowatoa Wasraeli katika nchi ya Misri. siku ya kumi na nne na ya kumi na tano ziko kariru na mwanzo wa mwezi wa Aprili katika kalenda ya Magharibi.

kwenye machweo.

"wakati wa jua kuzama"

Leviticus 23:7

Siku ya kwanza ni lazima mjitenge kwa pamoja

"Yawapasa kuitenga siku ya kwa kwanza ili kukusanyika pamoja" au "Ni lazima muione siku ya kwanza kuwa tofauti na kukusanyika pamoja.

mtamletea Yahweh matoleo ya chakula

Wataiwasilisha kwa Yahweh kwa kuteketeza juu ya madhabahu.

Siku ya saba ni ya kusanyiko takatifu lililotengwa kwa ajili ya Yahweh

Yale matakwa ambayo watu wanayakusanyikia katika siku hiyo yamezungumziwa kana kwamba siku hiyo ilikuwa kusanyiko. Kuwa umetengwa kwa Yahweh humaanisha kwamba wanapokusanyika, ni lazima wamwabudu Yahweh. : "Siku ya saba ni ambayo yawapasa kukusanyika pamoja ili kumwabudu Yahweh.

Leviticus 23:9

mganda wa nafaka wa matunda yake ya kwanza

"mganda wa kwanza" au "kitita cha kwanza cha nafaka."mganda" ni fungu moja la nafaka ambalo mtu amelifunga pamoja.

kwa kuwa litakubalika

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "kwa ajili yaaa kupokelewa na Yahweh" au "Nami nitalipokea"

Leviticus 23:12

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa yawapasayo watu kutenda.

sehemu mbili za kumi ya efa

Efa moja ni sawasawa na lita 22. "lita nne na nusu"

Moja ya nne ya hini

Hini moja ni sawasawa na lita 3.7. : "lita moja"

wala nafaka iliyokaangwa au nafaka mpya

wala nafaka iliyopikwa au isiyopikwa

Hii itakuwa amri ya kudumu katika vizazi vyote vya watu wenu

Tazama lilivyofafanuliwa katika 3:15

Leviticus 23:15

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa yawapasayo watu kutenda.

siku hamsini

"siku 50"

ya saba

Hii ni ya kwaida kwa namba saba

Leviticus 23:17

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumbia Musa yawapasayo watu kutenda

iliyotengenezwa kutokana na mbili ya kumi ya efa. Ni lazima ifanywe kwa unga laini na uliochanganywa na hamira

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. ; "uliyoitengenza kutokana na mbili ya kumi ya efa ya unga na ulioumliwa kwa hamira"

mbili ya kumi ya efa.

Takribani lita 4.5. : "lita nne na nusu"

na kutoa harufu nzuri ya kupendeza kwa Yahweh

Furaha ya Mungu kwa manukato huwakilisha fura furaha yake kwa watu wanaoteketeza matoleo hayo. : "naye Yahweh atapendezwa nanyi" au "impendezayo Yahweh"

Leviticus 23:22

Mtakapovuna mazao ya nchi yenu, Msivune kabisa kabisa pembeni mwa mashamba yenu

"Mkusanyapo mazao yenu, msiyakusanye yote hata kufika mipakani mwa mashamba yenu"

Leviticus 23:23

Katika mwezi wa saba., siku ya kwanza ya mwezi huo

Huu ni mwezi wa saba wa kalenda ya Kiebrani. Siku ya kwanza ni karibu na katikati ya mwezi wa Septemba kwenye kalenda ya Magharibi.

pumzika makini

kipindi cha wakati ambacho kilikuwa cha ibada na siyo kwa ajili ya kazi.

lazima mtoe dhabihu inayofanywa kwa moto kwa Yahweh

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yawapasa kutoa dhabihu mnayoifanya kwa mto kwa Yahweh" au "ni sharti mteketeze sadaka kwa Yahweh juu ya madhabahu"

Leviticus 23:26

siku ya kumi ya mwezi huu wa saba

Huu ni mwezi wa saba wa kalenda ya Ebrania. Siku ya kumi ni karibu na mwisho wa mwezi wa Septemba katika kalenda ya Magharibi.

siku ya upatanisho

Katika siku hii kila mwaka kuhani mkuu alifanya dhabihu kwa Yahweh ili kwamba Yahweh angeweza kusamehe dhambi zote za watu wa Israeli. : "siku ya dhabihu kwa ajili ya msamaha"

Leviticus 23:28

Maelezo Unganishi

Yahweh anaedelea kumwambia Musa yawapasayo watu kufanya kila mwaka.

azima akatiliwe mbali na watu wake

Tazama maelezo ya sura ya 7:19

Leviticus 23:30

Maelezo ya Kuunganisha

Yahweh anaendelea kumwambia mMusa yawapasayowatun kutenda.

katika siku hiyo

"katika siku ya upatanisho"

Hii itakuwa amri ya kudumu katika vizazi vyote vya watu wenu

Tazama katika sura ya 3:15

Sabato ya pumziko makini

Hii haikuwa Sabato ile ambayo waliishika kila juma katika siku ya saba. Hii ilikuwa ni sabato maalum katika siku ya upatanisho.

yapasa mjinyenyekeze

katika jambo hili, kujinyeyekeza wenyewe kulimaanisha kwamba wasingeku

  • la chakula chochote. Hii yweza kutmkwa wazi. : "Yapasa kujinyenyekeza wenyewe na msile kitu cho chote.

siku ya tisa ya mwezi

hii humaanisha mwezi wa saba katika kalenda ya Kiebrania. Siku ya tisa ni karibu na mwishoni mwa mwezi wa Septemba katika kalenda ya Magharibi. Hii yaweza kufanywa wazi. : "siku ya tisa ya mwezi wa saba"

Tangu jioni hata jioni

"Tangu machweo mpaka machweo kwenye siku inayofuata"

Leviticus 23:33

siku ya kumi natano ya mwezi wa saba

Hii ni karibu na mwanzoni mwa mwezi wa Oktoba katka lenda ya Magharibu.

Sikukuu ya Vibanda

Hii ni sherehe wakati ambao watu wa Israeli waliishi katika vibanda vya muda kwa siku saba kama njia ya kukumbuka muda walioutumia wakiishi kwenye jangwani baada ya kutoka Misri.

Leviticus 23:37

Hizi ndizo sikukuu zilizoamriwa

Sikukuu hizi zimetajwa katika 23:1-36

Leviticus 23:39

Kuhusu Sikukuu ya vibanda

Tazama katika sura ya 23:33

siku ya kumi natano ya mwezi

Huu ni mwaka wa saba wa kalenda ya Kiebrania. Siku ya kumi na tano ni karibu na mwanzoni na mwezi wa Oktoba kwenye kalenda Magharibi.

mmeyakusanya ndani matunda

"baada ya kuwa mmeyakusanya mazao"

Leviticus 23:40

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea na maelekezo yake juu ya sikukuu ya vibanda.

makuti ya mtende ... matawi ya mierebi kutoka chemchemi za maji

Matumizi ya matawi yanayoweza kuwa ni 1) kujenga vibanda vya muda au 2) kuyapunga kama sehemu ya kusherehekea kwa kwa shangwe, Baadhi ya tafsiri hutamkwa wazi matumizi yake; matoleomengine huacha kuesema uwazi wake.

Mierebi

Miti yenye majani marefu, membamba, ambayo huota karibu na maji.

Leviticus 23:42

wazao wenu, kizazi baada ya kizazi, waweze kujifunza

"kizazi baada ya kizazi" ni nahau inayomaanisha kwa kila kizazi kinachoishi baada ya kingine. "wazao wenu wa kizazi kijacho wwaweze kujifunza" au "wazao wenu wote waweze kujifunza daima"

Leviticus 24

Leviticus 24:1

Taarifa kwa Ujumla

Mungu anampa Musa maelekezo kuhusu vitu vya hekaluni

mafuta halisi yaliyokamliwa kutokana na mizeituni

"mafuta halisi ya zeituni

taa

Hii humaanisha ile taa au zile taa kwenye hema takatifu la Yahweh. hili laweza kufasiriwa kwa uwazi. : "ile taa katika hema la kukutania

Leviticus 24:3

Kauli Unganishi

Mungu anaendelea kumpa Musa maelekezo juu ya vitu katika hema la kukutania

Nje ya pazia lililoko mbele ya sanduku la maamzi

Kile kirai "sanduku la maamzi" huwakilisha ama zile mbao ziliandikwa juu yake au lile sanduka ambalo hizo mbao ziliwekwa ndani yake. Hivi vilitunzwa vema humo mahali patakatifu pa patakatifu, am bacho kilikuwa ni chumba nyma ya pazia ndani ya hema la kukutania. : "Nje ya pazia lililoko mbele ya mbao za sanduku la maamzi" au "Nje ya pazia

pazia

Hiki kilikuwa ni kitambaa kinene kilichoning;inizwa kama ukuta . hakikuwa kama pazia la dirishani la kitambaa chepesi.

tangu asubuhi hata jioni

tangu mawio mpaka machweo" au "usiku mzima"

Hii itakuwa amri ya kudumu katika vizazi vyote vya watu wenu

Tazama maelezo ya sura 3:15

Leviticus 24:5

Maelezo Ungajishi

Mungu anaendea kumwelekeza Musa juu ya vitu kwenye hema la kukutania

mbili za kumi za efa

Hizi ni kama lita 4.5. : "lita nne na nusu"

meza ya dhahabu safi mbele za Yahweh

Meza hii ilikuwa mahali pa takatifu, ambayo ilikuwa kabla ya patakatifu pa patakatifu.

Leviticus 24:7

Maelezo Ungajishi

Mungu anaendea kumwelekeza Musa juu ya vitu kwenye hema la kukutania

Mtaweka uvumba safi kando ya kila safu

Uvumba labda ulifuata baada ya mikate. : "yapasa muweke uvumba safi katika kila safu"

kuwa sadaka ya kuwakilish

Kile uvumba uliwakilishwa cha weza kutamkwa kwa uwazi> "ili kuwakilisha mikate kama sadaka" au kuwa sadak iwakilishayo mikate"

kwa kuwa ni sehemu ya matoleo

"kwa kuwa waliichukua kutoka kwenye matoleo"

matoleo kwa Yahweh yaliyofanywa kwa moto

"sadaka ya kuteketezwa kwa Yahweh" au "sadaka mnayoichoma kwa ajili ya Yahweh"

Leviticus 24:10

Sasa ilitokea

Kirai hiki kianunda sehemu mpya ya kitabu.

akalikufuru jina la Yahweh na kumlaani Mungu

Vilai vyote viwili kimsingi humaanisha kitu kimoja. "akamfufuru Yahweh kwa kumalaani" au alisema mambo maovu kumhusu Yahweh"

Shelomithi

Hili ni jina la mwanamke.

Dibri

Hili ni jina la mwaume.

Leviticus 24:13

Wale wote waliomskia wataweka mikono yao juu ya kichwa chake

Walikuwa waweke mikono yao juu ya kichwa chake kuonyesha kwamba alikuwa mwenye hatia.

Leviticus 24:15

Maelezo Unganishi

Mungu anaendelea kumwambia Musa walichopaswa kumtendea mtu aliyemkufuru Mungu

imempasa kubeba hatia yake mwenyewe

Kuteseka kwa ajili ya dhambi kumezungumziwa kana kwamba alikuwa mtu abebaye hatia yake. : "Sherti ateseke kwa ajili ya dhambi zake" au "ni lazima aadhibiwe"

lazima auawe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ni sharti watu watamuua" au "hakika yawapasa watu kumuua"

Leviticus 24:17

Maelezo Unganishi

Mungu anaendelea kumwambia Musa yawasayo watu kutenda mtu mwingine anapofanya mambo mabaya

ni lazima kwa hakika auewe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. "hakika yawapasa kumuua yeyote anayemuua mtu mwingine"

sharti amfidie

Jinsi anavyomfidia kwa weza kutamkwa wazi. : "yapasa amfidie kwa kumpa mwenye mali mnyama aliyehai"

uhai kwa uhai

Hii ni nahau inayomaanisha uhai mmoja ungechukua nafasi ya uhai mwingine. : "uhai mmoja kuchukua nafasi ya uhai mwingine" au "kumfidia yule aliyemuua"

Leviticus 24:19

Maelezo Unganishi

Mungu anaendelea kumwambia Musa yawasayo watu kutenda mtu mwingine anapofanya mambo mabaya

lazima atendewe vivyo hivyo

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "sharti mtende hivyo kwake"

Mvunjiko kwa mvunjiko

Virai hivi vinasisitiza kwamba mtu anapaswa kupokea madhara yale yalele ambayo yeye aliyafanya kwa mwingine.

jicho kwa jicho, jino kwa jin

Tazama aelezo ya sura 24:20

Jino kwa jino

Hii humaanisha jino lililong'olewa kutoka kinywani. : "kama anang'oa jino la mtu mwingine, mojawapo la meno yake litang'olewa" au iwapo anang'oa jino la mtu mwingine, nao watang'oa mojawapo ya meno yake"

Yera kwa jeraha

Hii humaanisha mifupa yenyekuvunjika. : Mfupa uliovunjika kaw amfupa uliovunkia" au "kamaanavunja mfupa wa , mmojawapo wa mifupa yake lazima uvunjwe " au "kama anavunja mfupa wa mtu mwingine, nao watavunja mmojawapo wa mifupa yake"

yeyote auaye mtu lazima auawe

Hii yaweza kutamkwa katika mtingo wa utendaji. : "nao sharti wamuue yeyote auaye mtu"

Leviticus 24:22

wakaitekeleza amri

"wakaitii amri"

Leviticus 25

Leviticus 25:1

hiyo nchi lazima ifanywe iwe ya kuishika Sabato kwa ajili ya Yahweh

Nchi inazunguziwa kana kwamba ilikuwa mtu ambaye angeweza kuitii sabato kwa kupumzika. Ni kama vile tu watu wanavyopaswa kupumzika kila siku ya saba, watu walikuwa waheshimu Mungu kwa kutoilima ardhi katika kila mwaka wa saba.: "yawapasa kuitii sheria ya Sabato kwa kuiacha ardhi ipumzike kila mwaka wa saba kwa ajili ya Yahweh" au "yawapasa uitii Sabato ya Yahweh kwa kutoilima ardhi kila mwaka wa saba"

Leviticus 25:3

mtaikatia matawi mizabibu yenu

Kuikatia matawi mizabibu ni kuyawezesha matunda kukua vizuri.

Sabato ya pumziko la utulivu kwa nchi itashikwa

Kutoilima ardhi nikumezungumziwa kana kwamba ni pumziko la nchi. Hii yawweza kukutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "yawapasa kuishika Sabato ya pumziko makini kwa ajili ya nchi" au "yakupasa kuitii sheria ya Sabato kwa kutoilima ardhi kila mwaka wa saba"

Leviticus 25:5

Hamtasimamia ... wanaoishi pamoja nawe mnaweza kujikusanyia chakula

Katika a 25:5-6 Yahweh anamaanisha hatamruhusu mmiliki wa shamba kuwasimamia wafanya kazi wake na kuivuna nchi kama afanyav miaka mingine sita. Hata hivyo, Yahweh atawaruhusu mtu mmoja mmoja kwenda shambani ili kuokota na kula mda wapatayo.

mizabibu yenu isiyokatiwa matawi

Hii humaanisha kwamba hayupo aliye angaliamizabibu na kukatia matawi kama wafanyavyo katika miaka sita mingine. Hii yaweza kutamkwa atika mtindo wa utendaji. : "mizabibu yenu msiyoikatia matawi"

Chochote ardhi isiyofanyiwa kazi itakachotoa

Chochote kipukacho juu ya ardhi isiyofanyiwa kazi"

ardhi isiyofanyiwa kazi

Hii humaanisha kwamba hakuna mtu aliyeziangalia bustani au mashamba kama wafanyavyo katika miaka sita mingine. Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "bustani zenu msizozitunza"

Chochote ardhi ... itakachotoa

"chochote kiotacho juu ya ardhi"

Leviticus 25:8

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa kiwapassacho watu kutenda.

kutakuwa na Sabato za miaka saba.

"kutakuwa na seti ya miaka saba"

miaka arobaini na tisa

miaka tisa - "miaka 49"

kumi ya mwezi wa saba

Huu ni mwezi wa saba wa kalenda ya Kiebrania. Siku ya kumi ni karibu na mwaisho mwezi wa Septemba katka kalenda ya Magharibi.

Siku ya Upatanisho

Tazama lilivyofasiriwa katia sura ya 23:26

Leviticus 25:10

mwaka wa hamsini

Hii ni namba ya mpango. : "mwaka wa 50"

Yubile kwa ajili yenu

Yubile ulikuwa mwaka ambao Wayahudi walipaswa kurejesha ardhi kwa wamiliki wake wa asili na kuwaacha huru watumwa. : "mwaka wa urejesho kwa ajili yenu" au "mwaka kwenu wa kurudisha ardhi na kuacha huru watumwa"

mali na watumwa ni lazima warejeshwe

Hii yweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "yawapasa kurudisha mali na watumwa"

Leviticus 25:11

Yubile kwenu

Tazama maelezo ya sura 25:10. Nayo yaweza kutamkwa wazi kwa waliyekuwa wakiirejesha hiyo ardhi. : "mwaka ambao mnapaswa kuirejesha ardhi kwangu"

Nanyi mtakula mazao yanayokua yenyewe kutoka mashambani

azama maelezo katika 25:5-7

Leviticus 25:13

mwaka huu wa Yubile

"mwaka huu wa urejesho" au "mwaka huu kurudisha ardhi na kuweka huru watumwa|"

Leviticus 25:15

Taarifa kwa Ujumla

MUngu anaendelea kumwambia Musa yawapasayo watu kutenda.

ambayo yaweza kuvunwa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "nayowea kuyavuna"

Yubile nyingine

"mwaka mwingine wa urejesho" au "mwakamwingine wa kurudisha ardhi"

Leviticus 25:18

muyatii maagiza, kuzitunza sheria zangu na kuzitekeleza

Virai hivi vyote humaanisha kitu kimoja. Zinasisitiza kwamba watu wanapaswa kutii kila asemalo Yahweh.

nanyi mtakula kiasi cha shibe yenu

Hii humaanisha kwamba wangekula vya kutosha mpaka matumbo yao yajae. : "mtakuala mpaka mjazwe" au mtakula tele"

Leviticus 25:20

Labda mtasema

"Mtasema" hapa humaanisha watu wa Israeli.

Nitaiamru baraaka yangu ije juu yenu

Mungu anaiongelea baraka yake kana kwamba ilikuwa mtu amabye angeweza kumtii yeye. "Nami nitaituma baraka yangu juu yenu" au "Nami nitawabariki ninyi"

kutoka kwenye riziki iliyohifadhiwa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "kutoka katika chakula mlichohifadhi"

Leviticus 25:23

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuzungumza

Ardhi haitauzwa kwa mmiliki mpya wa kudumu,

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. ; "Haipasi kuiuza ardhi yenu kwa kudumu kwa mtu mwingine"

lazima muitunze haki ya ukomboz

Jina "ukombozi" laweza kuelezwa na vitenzi "komboa" au "nunua tena ulichokiuza." : "yawapasa mkumbuke kwamba yule mmiliki wa asili anayo haki ya kuikomboa tena ardhi wakati wowote"

itawapasa kuruhusu ardhi inunuliwe tena na familia ambayo wewe uliinunua hiyo ardhi

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "lazima muiruhusu familia ile ambayo mliinunua ardhi kwao kuinunua tena hiyo ardhi"

Leviticus 25:26

ardhi hiyo ilipouzwa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "alipoiuza hiyo ardhi"

kurejesha kwa mtu aliyemuuzia fedha iliyosalia

Hii yaweza kuwekwa wazi. : "kuilipa hiyo fedha kwa mnunuzi aliyeinunu hiyo ardhi ambayo angekuwa amishailipa"

mwaka wa Yubile

Tazama lilivyotafsiriwa katika sura 25:10

ardhi itarejeshwa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Yule aliyeinunua hiyo ardhi atairejesha"

atarejea kwenye mali yake

"atarudi kwenye ardhi yake"

Leviticus 25:29

baada ya kuuzwa

"baada ya yeye kuiuza"

haki ya ukombozi

Ile nomino "ukombozi" yawaeza kuelezwa na vitenzi "komboa" au "nunua tena ulichokiuza." : "haki ya kukikomboa"

Kama nyumba hiyo haitakombolewa

Hii yaweza kutmkkwa katika mtindo wa utendaji. : "kama yeye au familia yake hwaikomboi hiyo nyumba"

Nyumba hiyo haitakuwa ya kurejeshwa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Mtu aliyeinunua nyumba hiyo hatatakiwa kuirejesha"

Mwaka wa Yubile

Tazama livyotafsiriwa kwenye mistari iliyotangulia.

Leviticus 25:31

Lakini nyumba za vijijini zisizokuwa na ukuta

Baadhi ya vijiji havikuwa na ukuta kuvizunguka.

Zaweza kukombolewa, na ni lazima zirejeshwe

"Mnaweza kuzinunua tena nyumba mlizoziuza, na wale waliozinunua sharti wazirejeshe hizo nyumba"

mwaka wa Yubile

Tazama ulivyofafanuliwa ktika mistari iliyotangulia katika sura hii

nyumba zinazomilikiwa na Walawi katika miji yao

"zile nyumba wanazozimiliki Walawi katika miji yao"

zaweza kukombelewa wakati wowote

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Walawi wanaweza kuzikomboa wakati wowote"

Leviticus 25:33

nyumba hiyo iliyouzwa katika miji ilimo, ni lazima irejeshwe

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Yyule aliyeinunua hiyo nyuma iliyoko mjini sharti airudishe "

mwaka wa Yubile

"mwaka wa urejesho" au mwaka wa kurudisha ardhi na kuacha huru watumwa"

miongoni mwa watu wa ni mali yao

Nchi ya Kanaani iligawanywa miongoni mwa watu wa Israeli, lakini katika hiyo, Walawi walikuwa wamepewa miji 48 tu pamoja na mashamba kuizunguka miji hiyo. : "sehemu ya ardhi yao ambayo Waisraeli wanaimiliki" au "mali yao katika nchi ya Israeli"

Lakini yale mashamba yanayozunguka miji yao hayataweza kuuzwa

"Lakini Walawi hawatauza hayo mashamba yanayozunguka miji yao"

Leviticus 25:35

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwambia Musa yawapasayo watu kutenda.

Usimtoze riba

Usimfanya akulipe zaidi ya ulichomkopesha yeye"

Leviticus 25:39

hutamfanyisha kazi kama mtumwa. Mtendee kama mtumishi wa kuajiriwa.

Hii humaanisha kwamba mmiliki alikuwa amtendee Mwisraeli kwa heshima kuliko vile ambavyo angelimtendea mtumwa.

Mwaka wa Yubile

Tazama maelezo katika 25:33

Leviticus 25:42

Maelezo Unganishi

Mungu anaendelea kumwambia Musa yaliyompasa kuwaambia watu.

wao ni watumishi wangu

"wananchi wenzako ni watumishi wangu"

Hawatauzwa kama watumwa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Haiwapasi kuwauza kama watumwa.

waweza kununua watumwa kutoka kwao.

"labda mwaweza kununua watumwa kutoka kwa mataifa hayo"

Leviticus 25:45

mgeni, -a kigeni, mpitaji

Tama maelezo katika sura zilizotangulia

Familia

Ule msemo "familia" humaanisha kikundi cha watu wanaohusiana kwa damu na kwa kawaida huhusisha baba, mama, na watoto wao. Mara kwa mara pia huhusisha ndugu wengine kama vile babu na bibi, wajuu, wajomba na shangazi. . Familia ya Kiebrania ni jamii ya kidini inayopitia chini ya mapokeo chini ya ibada na maelekezo. . Familia pia yaweza kujumuisha watumwa, masuria, na hata wageni. Baadhi ya lugha zaweza kuwa na nenonpana kama vile "ukoo" au "kaya" ambalo linaweza kufaa vema katika mazingira ambayo huhusisha zaidi ya wazazi, na watoto tu . . Ule msemo "familia" pia umetumika kumaanisha watu wanaohusiana kiroho, kama vile watu waliosehemu ya familia ya Mungu kwa sababu wanamwamini Yesu.

Watoto, mtoto

Katika Biblia ule msemo "mtoto" mara kwa mara umetuka kwa ujumla kumaanisha mtu mwingine aliye mdogo kiumri, pamoja na mtot mchanga. Ule msemo "watoto" ni mtindo wa wingi nao pia una maana nyingi za kitamathali.

. Katika Biblia, wale wanafunzi au wafuasi wakati mwingine wanaitwa "watoto" . Mara kwa mara ule msemo "watoto" limetumika kuamanisha mzao wa mtu . Kile kirai "wana wa" chaweza kumaanisha wale wanaoelezewa na kitu fulani. Baadhi ya mifano hii yaweza kuwa . watoto wa nuru . watoto wa kutii . watotowa mwovu . Msemo huu waweza pia kumaanisha watu ambao wako kama watoto wa kiroho. Kwa mfano, "watoto wa Mungu" humaanisha watu wa Mungu kupitia imani katika Yesu.

rithi, urithi, mirathi, mrithi.

Ile misemo "rithi" ana "urithi" humaanisha kupokea kitu fulani cha thamani kutoka kwa mzazi au mtu mwingine kwa sababu ya uhusiano maalum na mtu huyo. "Mrithi" ni mtu anayepokea urithi.

. Urithi wa kuonekana unaopokelewa waweza kuwa fedha, ardhi, au aina nyine ya mali. . Urithi wa kiroho ni kila kitu ambacho Mungu huwapa watu wanaoamini katika Yesu, ikiwa ni pamoja na baraka katika maisha haya pia na uzima wa mile na kukaa paoja naye.

. Pia Biblia inawaita watu wa Mungu kuwa ni hurithi wake, ambapo humaanisha kwamba wao ni wake yeye, wao ni miliki yake ya thamani.

. Mungu alimwahidi Abrahamu na wazao wake kwamba wangerithi nchi ya Kanaani, nayo ingekuwa yao milele.

. Pia kuna maana ya kitamthali au kiroho ambamo kwayo watu wa Mungu wametajwa kuwa "watairithi nchi." Hii humaanisha kwamba wao watastawi na kubarikiwa na Mungu katika njia zote mbwili kimwili na kiroro

. Katika Agano Jipya, Mungu anaahidi kwamba wale wanaomtegemea Yesu "watarithi wokovu" na "kurithi uzima wa milele." Pia imeelezwa kuwa, ni kurithi ufalme wa Mungu." Huu ni urithi wa kiroho udumuo milele. . Kuna maana nyingine za kitamathali za misememo hii

. Biblia husema kwamba wale watu wenye hekima watarithi "utukufu" na watu waliowanyoofu "watarithi mambo mema"

. "Kurithi ahadi" humaanisha kupokea mambo mema ambayo Mungu ameahidi kuwapa watu wake.

. Musemo huu pia umetumika katika maana hasi ikiwarejelea watu wapumbavu au wasiotii "watakaorithi upepo" au watakorithi "upumbavu." Hii humaanisha kwamba wanapokea matokeo ya matendo yao maovu, pamoja na adhabu maisha yasiyo na maana.

ndugu

Msemo huu "ndugu" mara kwa mara humaanisha mtu mwanaume anayeshirikiana na mtu mwingine angalau mzazi mmoja kiukoo.

. Katika Agano la Kale, msule msemo "ndugu" pia umetumika kama uhusiano wa jumla kwa jamaa kama vile washirika wa kabila, ukoo, au wa kikundi kimoja.

. Katika Agano Jipya, mara kwa mara Mitume waliutumia "ndugu" kumaanisha Mkriso mwenzako, likijumuisha wote wanaume na wanawake. kwa kuwa Waminio katika Kristo wote ni washirika wa familia moja ya kiroho, na Mungu akiwa Baba yao wa mbinguni.

. Mara chache katika Agano Jipya mitume walitumia msemo "dada" walipomaanisha Mkristo mwanamke moja kwa moja, au kusisitiza kwamba wote, wanaume na wanawake wamehusishwa. Kwa mfano, Yakobo anasisitiza kwamba anaporejelea "kaka" na "dada" anyehitaji chakula au nguo, atakuwa nazungumzia waamini wote.

MAPENDEKEZO YA UFASIRI

kikundi cha watu, watu, watu wa,

Tazama maelezo ya sura ya 18:1-3

Israeli, Waisraeli, taidfa la Israeli

Ule msemo "Israeli" in jina ambalo Mungu alimpa Yakobo, linamaana ya, "yule apambanaye na Mungu

. Wale wazao wa Yakobo walikuja kujulikana kama "watu wa Israeli," taifa la Ireaweli," au "Waisraeli."

. Mungu aliunda agano lake na watu wa Israeli. Walikuwa watu wake wateule.

. Tifa la Israeli liliundwa na makabila kumi na mbili. . Mara tu baada ya mfale Sulemani kufa, Israeli iliganyika katika falme mbili: ufalme wa Kusini uliitwa "Yuda" na ule uflamue wa Kaskazini uliitwa Israeli.

. Mara zote ule msemo "Israeli" waweza kutafsiriwa kuwa, "watu wa Israeli," au ""taifa la Israeli," kulingana tu ma mazingira.

Leviticus 25:47

baada ya Mwisraeli mwenzako kuwa amenunuliwa, anaweza kurejeshwa kwa maliopo. Mtu mwingine katika familia yake anaweza kumkomboa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Baada ya mgeni kumnunua Mwisraeli mwenzako mtu mwingine katika familia ya Mwisraeli aweza kumnunua tena aliyekuwa ameuzwa>

Leviticus 25:49

mpaka mwaka wa Yubile.

Mwisraeli angeweza kuwa mtumwa mpaka mwaka wa Yubile. Haya maelekezo ni kwa ajili ya Mwisiraeli alipotaka kuununua tene uhuru wake kabla ya mwaka wa Yubilee.

mwaka wa Yubile

Tazama maelezo katika sura zilizotangulia

kulingana na kiwango cha mendshahara anaolipwa mtumishi aliyeajiriwa

Endapo Mwisraeli anaununua tena uhuru wake, yule mgeni angeweza kukodi mtumishi ili kufanya zile kazi ambazo mwisraeli angekuwa amezifanya lakini haitakuwa hivyo. Vile vitenzi "kulipwa" na "ajiriwa" zaweza kuelezwa katika mtindo wa utendaji. : "kulingana na kiwango ambacho mtu angelipa ili kukodi mtumishi"

kwa idadi ya miaka ambayo angeweza kuendelea kufanya kazi

kwa idadi ya miaka kufikia Yubileeambayo huyo Mwisraeli angekuwa ameendelea kufanya lakini ameacha.

Leviticus 25:51

atalazimika kulipa

"huyo Mwisraeli atalazimika kurejesha"

Leviticus 25:53

:hatendewi kwa ukatili

"Huyo mgeni aliyemnunua yeye kama mtumwa itampasa kumtendea yeye."

hatendewi kwa ukali

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "hakuna amtendeaye yeye viba"

Iwapo hakukombolewa katika njia hizi

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaj, na ile naye ni lazima akombolewe kutoka yaweza kutamkwa wazi. : "Kama hayupo wa kumkomboa yeye kwa njia hizi kutoka kwa aliyemnunua kama mtumwa."

kwa njia hizi,

"katika njia hizi"

atatumika mpaka mwaka wa Yubile, yeye pamoja na watoto wake

MWisraeli mtumwa pamoja na wa watoto wake watamtumikia mgeni mpaka mwaka wa Yubile., kisha huyo Mgeni angepaswa kumwacha huru Mwisraeli huyo pamoja na watoto wake.

Kwangu mimi watu wa Israeli ni watumishi

"Kwa kuwa ni kwamba kwangu watu wa Israeli ni wa tumishi." Hii nis sababbu kwamba Mungu alitaka Waisraeli waachwe huru katika mwaka wa Yubile. Walikuwa watumishi wake. Walikuwa hawaruhusiwi kuwa wa tumwa wa mwingine wa kudumu pia.

Leviticus 26

Leviticus 26:1

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa yawapasayo watu kutenda.

muzitunze Sabato zangu

"tiini sheria kwa ajili ya Sabato zangu"

Leviticus 26:3

mtatembea katika sheria zangu na kuzishika amri zangu na kuzitii

Kuna njia tatu za kuseama jambo lile lile. Yote husisitiza kwamba ni lazima watu watii kila kitu anachowaamru Mungu kufanya. "kama mtazitii kwa uangalifu sheria na amri zangu"

mtatembea katika sheria zangu

Mwenendo kulingana na sheria umezungumziwa kana kwamba ulikuwa kutembea katika sheria. : "kama mtaenenda kulingana na sheria" au "kama mtaishi kulinga na sheria zangu"

Leviticus 26:5

mtakula mkate na kushiba na kuishi

Mkate hapa huwakilisha chakula. "Hata ukamilifu" humaanisha hata matumbo yao lijazwa kwa chakula. : "mtakula chakula mpaka mmejazwa" au "mtakuwa na chakula telea chakula"

Nami nitatoa amani katika nchi

"Huko nitasababisha kuwa amani katika nchi"

upanga hautapita katika nchi yenu

Hapa "upanga" huwakilisha majeshi ya adui" au "majeshi yatawashambulieni"

Leviticus 26:7

nao wataanguka mbele yenu kwa upanga

"Kuanguka" hapa huwakilisha kufa, na "upanga" huwakilisha ama kushambulia watu kwa upanga au vita kwa ujumla"

Watu wenu watano watafukuza adui mia moja, na watu wenu mia moja watafukuza adui elfu kumi

Hii humaanisha Waisraeli watakuwa na ushindi dhidi ya majeshi makubwa.

tano ... mia moja ... elfu kumi

"5 ... 100 ... 10,000"

Leviticus 26:9

Nitawatazama kwa upendeleo

"Nitawaonyesha upendeleo" au "Nitawabariki nyinyi"

kuwafanya nyinyi mzae na kuwazidisha nyinyi

Virai hivi viwili vinamrejerelea Mungu akiwasababisha wao kuwa na wazao wengi kwa hiyo wanakuwa kundi kubwa.

kuwafanya nyinyi mzae

Mungu anakuzungumzia kuwa na watoto kwao kana kwamba walikuwa miti izaayo matunda mengi. : "nitawasababisha kuwa na watoto wengi"

Mtakula chakula kilichotunzwa ghalani kwa muda mrefu

"Mtakuwa na chakula kilichohifadhiwa ghalani cha kutosha kula kwa muda mrefu" au "Mtakuwa na chakula cha kutosha kuhifadhi ghalani na kukila kwa muda mrefu"

Leviticus 26:11

Nitaliweka hema langu katikati yenu

"Nitaweka mahali pa makao yangu miongoni mwenu"

Nami sitachukizwa nanyi

"Nitawakubali ninyi"

Nitatembea miongoni mwenu

"Nami nitawakubali ninyi"

Nimevunja makomeo ya nira yenu

Mungu anauzungumzia utumwa wao kana kwamba kulikuwa ni kuvaa nira ambayo huivaa wanyama ili kufanya kazi ngumu. Kuvunja makomeo ya nira huwakilisha kuwaweka wao huru. : "Nimewaweka huru kutoka katika kazi ngumu walizowalazimisha kuzifinya"

Leviticus 26:14

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anamwambia Musa kitakachotokea endapo watu wazitii mamri zake.

Leviticus 26:16

kama mtafanya mambo haya

Kila kirai "mambo haya" hurejelea mambo yaliyoorodheswa katika sura 26:14

Nitasababisha hofu juu yenu

Hapa "hofu" huwakilisha mambo yatakayowasababisha wao kuhofu. : "Nami nitatuma maafa yatayowaogofya ninyi"

kuondoa uhai wenu

"Nitayaondoa taratibu maisha yenu" auNitaninyi mfe pole pole" . Ni yale magonjwa na homa yatayofanya hivi.

Mtapanda mbegu zenu kwa hasara

Kile kirai "kwa hasara" humaanisha wasingepata kitu cho chote kutoka kwenye kazi zao. ; "Nanyi mtazipanda mbegu zenu bila faida" au "Nanyi mtazipanda mbegu zenu, lakini hamtapata kitu cho chote kutoka kwake"

Nitakaza uso wangu dhidi yenu

Hii humaanisha kwamba atakuwa kinyume nao. Uso wake utaonyesha ghadhabu yake naye atapigana dhidi yao.: "Nitakuwa mpinzani kwenu" au "nitakua kinyume chenu"

na mtashindwa na adui zenu

: "adui zeny watawashinda ninyi"

Leviticus 26:18

mara saba

Neno "saba" hapa siyo halisi. Humaanisha Yahweh atazidisha ukali wa adhabu yake.

Nami nitakivunja kiburi chenu

Kule kutumia nguvu lili kuwafanya wao wasiwe na kiburi kumezunguziwa kana kwamba alikuwa avunjje kiburi chao. : "Nami nitaadhibu na kwa hiyo nitakomesha kiburi unachojisikia kuusiana na nguvu zenu" na "nitawaadhibu ili kwamba msiwe na kiburi tena kwa sababu ya nguvu zenu.

Nitaifanya mbingu juu yenu iwe kama chuma na nchi yenu kama shaba

Hii humaanisaha Mungu ataizuia mvua isidondoke kutoka mawinguni. Hii itaifanya ardhi kuwa ngumu kiasi kwamba watu hawataweza kupanda mbegu au kukuza mazao.

Nguvu yenu itatumika bure

Kule kufanya kazi kwa nguvu kumezungumziwa kana kwamba kulikuwa kutumia nguvu zao ha hawa kuwa na nguvu tena. Kile kirai "bure" humaanisha kwamba wasingepata kitu kutokana na kazi kufanya kazi kwao kwa juhudi kubwa. : "Nanyi mtafanya kazi kwa juhudi sana bila mafanikio" au mtuafanya kazi kwa juhudi sana, lakini hamtapata kila kitu chema kutokana na kufanya kazi kwa juhudi sana"

Leviticus 26:21

enenda kinyume changu

Kuenenda huwakilisha tabia. Kuenenda kinyume na Mungu huwakilisha kumpinga au kumwasi Yeye. "Asi dhidi yangu"

nitaleta mapigo mara saba zaidi juu yenu

Ile nomino dhahania "mapigo" yaweza kutamkwa kama kitenzi "gonga." "Nitawagonga kwa wingi zaidi mara saba

nitaleta mapigo mara saba zaidi juu yenu

Kule Yahweh kusababisha maafa kutokea kwa Waisraeli kumezungumziwa kana kwamba angewapiga na mapigo au kuwagonga. : "Nitasabisha maafa mengi yaje mara saba dhidi yenu" au "Niitawaadhibu kwa ukali zaidi mara saba"

mara saba

Hapa "mara saba" siyo halisi, humaanisha Yahweh atazidisha ukali wa adhabu yake.

sawasawa na dhambi zenu

Ile nomino "dhambi" yaweza kuelezewa pamoja na kitenzi "tenda dhamb.i." : "kulingana na mara mlizotenda dhambi"

ambao watawaibia watoto wenu

Kuiba huwakilisha kuwavamia au kuvamia na kuwaburuta. : "watakaowavamia nyinyi na kuwaburuta watoto wenu"

Hivyo barabara zenu zitakuwa jangwa.

"Ili kwamba hatakuwepo wa kusafiri kwaenye barabara zenu." "Kuwa jangwa" humaanisha kwamba hakuna mtu yeyote huko.

Leviticus 26:23

Endapo pamoja na mambo haya

"Iwapo nitaadhibu ninyi kama hivi" au 'Iwapo nitawwadibisha ninyi kama hivi na"

msiyakubali marekebisho

Kukubali marekebisho yake huwakkilisha kuitikia kwake kwa usahihi. Katika jambo hili kuitika kwa usahihi kwake ni kuchagua kumtii Yeye. : "bado hamsikilizi marudi yangu" au "bado hamtaki kunitii Mimi"

kuenenda katika upinzani dhidi yangu

Kuenenda huwakilisha tabia. Kuenenda kinyume chake humaanisha kumpinga Yeye au kupigana dhidi Yake. : "kunipinga" au "pigana dhidi yangu"

nami pia nitaenenda kinyume chenu

Kuenenda huwakilisha tabia. Kuenenda kinyume chao humaanisha kuwapinga au kupigana dhidi yao. : "Pia Nami nitapigana dhidi yenu"

Mimi mwenyewe nitawaadhibu mara saba

Namba 7 huwakilisha ukamilifu. : "Mimi mwenyewe binafsi nitawaadhibu mara nyingi" au "Mimi mwenyewa nitawaadhibu kwa ukali wa hali ya juu"

kwa sababu ya dhambi zenu

le nomino dhambi yaweza kuelezewa na kitenzi "tenda dhambi." : "kwasababu mnaendelea kutenda dhambi dhidi yangu"

Leviticus 26:25

Nitaleta upanga juu yenu

Hapa "upanga" huwakilisha jeshi au shambulizi kutoka kwa jeshi. : "Nitaleta jeshi la adui dhidi yenu" au "nitasababisha jeshi la adui kuwavamia nyinyi"

utakaowaadhibu kwa kisasi

"amabao utawaadhibu nyinyi"

kwa sababu ya kulivunja agano

"kwa kutotii agano" au "kwa sababu hamlitii agano"

Nanyi mtakusanywa pamoja

Hii yaweza kutamkwa katika mtingo wa utendaji. : "Mtakusanyika pamoja" au "Mtajificha"

nanyi mtachukuliwa mikononi mwa adui yenu

Hapa " mikononi" humaanisha "kwenye udhibiti" na humaanisha kushindwa na adui. Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "adui zenu watawashindeni"

Nitakapokomesha mgao wa chakula,

Kule kukiharibu chakula ambacho watu wamikitunza au kuwafanya watu wasikipate kumezungumziwa kana kwamba kukata uwaji wa chakula. : "Nitakapoharibu chakula mlichokihifadhi" au "Nitakapowazuia msiweze kupata chakula"

wanawake kumi wataweza kuoka mkate wako kwenye chombo kimoja cha kuokea

Hii hudokeza kwamba kutakuwa na unga kidogo sana kiasi kwamba chombo kidogo sana cha kuokea kitaweza kubeba mikate yote ambayo wanawake wengi wateza kuweka ndani yake.

watakugawia mkate wako kwa uzani

Hii humaanisha kwamba kutakuwa na chakula kidogo sana watatakiwa kukipima ni kiasi gani kila mtu anapata.

Leviticus 26:27

Endapo hamtanisikiliza

Kusikliza huwakilisha yale aliyoyasema. : "kama hamnitii mimi"

kuenenda kinyume na mimi

Tazama maelezo katika mistari iliyotangulia katika sura hii.

nitakwenda kinyume nanyi

Tazama maelezo katika mistari iliyotangulia katika sura hii.

Nami nitawaadhibu hata mara saba

Tazama maelezo katika mistari iliyitangulia katia sura hii.

Leviticus 26:29

Nitapaangamiza ... kuziangusha ... kuzitupa maiti zenu

Kwa sababu Mungu atatuma jeshi kufanya mambo haya, anazungumzia kana kwamba atayafanya. : "Nitatuma jeshi ala adui ili kuangamiza ... kuangusha chini ... kutupa maiti zenu"

maiti zenu

"mizoga ya miili yenu"

maiti za sanamu zenu

Mungu anazungumzia sanazisizo na uhai kana kwamba zilikuwa na uhai na kisha zikafa. : "sananmu zenu zisizo na uhai"

Leviticus 26:31

Nitaigeuza miji yennu kuwa magofu na kupaharibu patakatifu penu

Kwa sababu Mungu angetuma majeshi kufanya mambo haya, anasungumza kana kwamba angeyafanya yeye mwenyewe. : "Nitatuma majeshi ya maadui ili kuigeuza miji yenu magofu na kuziharibu madhabahu zenu"

patakatifu penu

Kullikuwa na mahali ambapo watu waliabudu sanamu badala ya Mungu.

Nami sitapendezwa na harufu nzuri ya matoleo yenu

Kwa kawaida Bwana kufurahisha na harufu nzuri huwakilisha kule kufurahishwa kwake na wanaoteketeza hizo sadaka, lakini katika hili, watu wangaliteketeza sadaka zao, lakini Mungu asingependezwa nao. : "Nanyi mteteketeza sadaka zenu, lakini stapendezwa nanyi"

Nitaufuta upanga wangu na kuwafuatia

Hii huwakilisha utumaji wa majeshi ili kuwavamia. "Nitatuma majeshi ya maadui ili kuwashambulia nyinyi" au "Nitatuma majeshi ya maadui ili kuwashambulia nyinyi kwa mapanga"

Nchi yenu itatelekezwa, na miji yenu itakuwa magofu

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "nany mtaitelekeza nchi yenu , nao adui zenu wataiharibu miji yenu"

Leviticus 26:34

Nayo nchi itazifurahia Sabato zake

Hao watu walipaswa kuitii sheria ya Sabato kwa kutoilima ardhi kila mwaka wa saba. Mungu anazungumzia juu ya hili kana kwamba ardhi ilikuwa mtu ambaye angalitii sheria ya Sabato na kupuzika. : "Kisha nchi itapumzika kulingana na sheria ya Sabato" au "Kisha, kama inavyotakiwa na sheria ya Sabato, ardhi haitalimwa"

nchi itapumzika

Mungu huzungumzia juu ya nchi kutolimwa kana kwamba alikuwa mtu ambaye angepumzika, : "haitalimwa"

Nitatuma hofu ndani ya mioyo yenu

Kutuma hofu myoyoni mwao huwakilisha kuwafanya wao waogope"

kana kwamba mlikuwa mkikimbia mbele za upanga

Upanga huwakilisha ama mtu mwingine aliyekuwa tayari kuua akitumia upanga au shambuzi kutoka kwa jeshi la adui. : "kana kwamba mlikuwa mkitoroka mtu mwingine aliyekuwa akiwafukuza na upanga" au kana kwamba mlikuwa mkilitorka jeshi la adui"

Leviticus 26:37

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuelezea kitachotokea kwa Waisraeli watakapolazimisha kwenda mataifa ya adui zao.

kana kwamba mlikuwa mkiukimbia upanga

Tazama maelezo kuhusu upanga na uwakilishi wake katika mistari iyotangulia

kusimama mbele za aduii zenu

Kusimama mbele za adui huwakilisha kuanguka adui wanawapovamia na kupigana dhidi yao. : "kuwazuia adui zenu wanawavamia ninyi" au "kujibu mapigo dhidi ya adui zenu"

nayo nchi ya adui zenu yenyewe itawamezeni

Yahweh anaongelea kuhusu nchi ya maadui kana kwamba ilikuwa mnyama pori ambaye angewala Waisraeli. Lile neno "meza" husisitiza kwamba wengi wa Waisraeli watafia huko. : "matfia katika nchi ya adui zenu"

Wale watakosalia miongoni mwenu

"Wale wa kwenu ambao wasiokufa"

wataangamia katika dhambi zao

Kuangamia katika dhambi zao huwakilisha kuangamia kwa sababu ya dhambi zao.

dhambi za baba zao

Hapa "za baba zao" huwakilisha wababu wao

Leviticus 26:40

kugeuka dhidi yao

Hii huwakilisha kuwapinga> : "kuwapinga wao"

iwapo mioyo yao isiyotahiriwa itanyenyekezwa

Hapa ule msemo "mioyo isiyotahiriwa" humaanisha nafsi nzima. : " kama wao watakuwa wanyenyekevu badala ya kukaidi kwa ushubavu"

nami nitalikumbuka agano langu na Yakobo, agano langu na Isaka, agano langu na Abrahamu

"Kukumbuka " ni nahau inayomaanisha kukumbuka kwa makusudi. Hapa inawakilisha kutimiza agano lake. : "kisha nitatimiza agano nililofanya na Yakobo, Isaka na Abrahamu"

nitaikumbuka nchi

"Kukumbuka " ni nahau inayomaanisha kukumbuka kwa makusudi." Hapalinawakilisha nchi. : "Nitatimiza ahadi yangu juu ya nchi"

Leviticus 26:43

Nayo nchi itakuwa imetelekezwa na wao

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Watu wa Israeli waitelekeza nchi yao"

Leviticus 26:44

nitalikumbuka agano langu na baba zao

: "Nitatimiza agano langu na babu zao.

Maelezo kwa Ujumla

Hili lina hitimisha ujumbe wa Yahweh kwa Musa katika mlima wa Sinai kuhusiana na baraka kwa utii na adhabu kwa kutotii.

machoni pa mataifa

Hii huwakilisha ufahamu wa mataifa. ": "katika ufahamu wa mataifa" au "nayo mataifa yajue kuhusu hili"

mataifa

Hili huwakilisha watu wa mataifa. "machoni pa watu wa mataifa"

Leviticus 26:46

amru, kuamru, amri

Ule msemo "amru" humaanisha kumwagiza mtu mwingine kufanya jambo fulani. "Agizo" au "amri ni kile mtu aliagizwa kufanya.

. Ingawaje misemo hii yote inamaana moja kimsingi, maraa kwa mara "amri" hurejelea maagizo fulani ya Mungu amabayo yako rasmi zaidi na ya kudumu, kama vile "amri kumi"

. agizo laweza kuwa chanya ("Heshimu wazazi wako") au hasi ("Usiibe")

. "Kuchukua amri" humaanisha "kuchukua udhibiti" au "shika madaraka" ya kitu kitu fulani au mtu mwingine.

Agizo

Agizo ni tangazo au sheria amabayo hutangazwa hadharani kwa watu wote. . Sheri za Mungu pia huitwa maagizo, masharti au amri. . kama vile sheria na amri, maagizo lazima yatiiwe

. Mfano wa agizo lililotolewa na mtawala mwanadamu ni lile tangazo lililotolewa na Kaisari Augusto kwamba kila aliyekuwa akiishi katika Dola la Kirumi lazima arudi katika mji wa nyumbani kwao apate kuhesabiwa kwenye sensa.

. Kuagia kitu fulani humaanisha kutoa amri ambayo lazima itiiwe. Hii ingeliweza kutafsiriwa kama, "kuagiza" au "kuamru" au "kudai kirasmi" au kutengeneza sheria hadharani."

. Jambo fulani "lililotangazwa" kutokea humaanisha kwamba hakika hili litatokea. au lililokwisha kusudiwa na halitabadilishwa" au "limetangazwa kabisa kabisa kwamba litatokea."

sheria, sheria ya Musa, sheria ya Mungu, sheria ya Yahweh

Misemo hii yote hurerjea amri na mfundisho ambayo Mungu alimpa Musa kwa ajili ya Waisraeli kuzitii. Ile misemo "sheria" na sheria ya Mungu" kwa ujumla pia imetumika kumaanisha kila kitu ambacho Mungu anawatakawatu wake kutii. . Kwa kutegemeana na muktadha, sheria yaweza kumaanisha: . zile amri kumi ambazo aliziandika kwenye mbao za mawekwa ajili ya Waisraeli. . sheria zote alizopewa Musa . vile vitabu vitano vya kwanza vya Agano la Kale. . Agano la Kale lote (pia hurejelewa kama "maandiko" katika Agano Jipya. . Mafundisho yote na maenzi ya Mungu . Kile kirai" sheria na manabii" katika Agano Jipya kimetumika kumaanisha maandiko ya Kiebrania (Agano la Kale)

Sinai, Mlima Sinai

Mlima sSinai ni jina la mlima ambao huenda kulikuwa upande wa eneo linaitwa kwa sasa rasi ya Sinai. Pia lilijulikana "Mlima Horebu." . Mlima Sinai ni sehemu kubwa ya jangwa lenye miamba. Waisraeli walikuja kwenye Mlima Siani walipokuwa wakisafiri kutoka Misri kwenda kwenye Nchi ya Ahadi. . Mungu alimpa Musa zile amri kumi juu ya Mlima Siani

Leviticus 27

Leviticus 27:1

Iwapo mtu yeyote anatoa kiapo maalum cha kuwa mnathiri kwa Yahweh

Katika jambo hilikiapo kingehusisha kujito mwenyewe au mtu mwingine kwa Mungu. Hii yaweza kutamkwa wazi. : "Kiwa mtu fulani anaapa kmtoa mtu mwingine kwa Yahweh"

tumieni tathmini zifuatazo

Badala ya kumpa mtu, yeye ndiye angempa Bwana kiasi fulani cha cha fedha. : "Tumieni thamani fulani kama zawadi yenu kwa Bwana kwanya nafasi ya mtu" au mpeni Bwana kiasi kifuatacho cha fedha badala ya mtu"

Leviticus 27:3

tumieni tathmini zifuatazo viwe viiwango vyenu vya thamani

"Kiasi cha kulipa" au yapasa ulipe"

Ishirini ... sitini ... hamsini ... thelathini

"20 ... 60 ... 50 ... 30"

shekeli hamsini za fedha

Kama ni laziam kutumia vipimu vya uzani vya kisasa, hapa kuna nhia mbili kufanya hilo. "vipand hamsini vya fedha, ambacho kila kimoaja hupima gramu kumi" au "gramu mia tano za fedha"

kulingana na vipimo vya shekeli ya mahali pa patakatifu

Hizi zikikuwa shekeli za vipimo mbali mbali. Hii ni njia moja ambayo mtu alikuwa atumie kwenye hema takatifu. Kilipima gramu 11. : Tumie aina ya shekeli inayotumika kwenye hema la kukutania" au "mnapopima fedha, tumieni ni kipimo amabacho hutumika kwenye hema.

shekeli thelathini

: "vipande thelathini vya fedha, ampao kila kimoja hupima gramu kumi" au "shekeli thelathini sawasawa na gramu mia tatu"

Leviticus 27:5

tano ... ishirini ... kumi ... tatu

"5 .. 20 ... 10 ... 3"

viwango vyenu

"kiasi cha kulipa' au yapasa mlipe"

shekeli ishirini

: "vipande ishirini vya fedha" au "gramu mia mbili za fedha"

na kwa mwanamke ni shekeli kumi

Kirai "umri huo" na "viwango vyenu vya thamani vitakuwa" ni vimeachwa wazi viweze kuelekweka. : "naye mwanamke wa umri huo lazima viwango vyenu vya thamani viwe shekeli kumi"

shekeli kumi

"vipande kumi vya fedha" au gramu hamsini za fedha"

shekeli tano za fedha

"vipande vitano vya fedha" au gramu mia moja za fedha"

shsekeli tatu

"vipande vitatu vya fedha" au gramu thelethini za fedha"

Leviticus 27:7

miaka sitini na zaidi

"umri wa miaka sitini na wazee"

Sitin ..kumi na tano .. kumi

"60 ... 15 ... 10"

shekeli kumi na tano

"vipande kumi na tanovya fedha" au "gramu 150 za fedha"

huyo mtu anayetolewa lazima atapelekwa kwa kuhani

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "atampeleka kwa kuhani huyo mtu anayemtoa"

Leviticus 27:9

atatengwa kwake.

"atangwa kwa Yahweh"

hao wawili; yule anayetolewa na yule anayebadilishwa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "wote wawili huyo aliyetolewa na yule anayembadilisha" au " mnyama naweza kumaanisha kuwa "wanyama wote wawili"

Leviticus 27:11

kwa uhalisia siyo kisafi, kwa hiyo, Yahweh hatakikubali

Mnnyama amezungumziwz kana kwamba alikuwa mchafu kimaumbbile. Anaweza kuwa najisi kwa sababu ni anina fulni ya mnyama au kwa sababu ana kasoro. .: kwa uhalisia ni yule ambaye Yahweheh hatampokea"

thamani ya soko

Hii ni thamani ambayo mnyama huwa thamani tu anamnunua au kumuuza.

anapenda kumkomboa

anapena kumrejesha kwa kumnunua tena"

Leviticus 27:14

atalazimika kuongeza sehemu ya tano ya thamani yake kwenye gharama ya

"ya tano ni sehemu ya kitu fulani iliyowanywa katika sehemu tano zilizo sawa kwa kila moja ya sehemu hizo, na kuilipa yote"

Leviticus 27:16

kiasi cha mbegu inayotakiwa kuipanda katika ardhi hiyo

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "kile kiasi cha mbegu mtu angehitaji kupanda"

homeri moja ya mbegu za shairi ambayo itathamanishwa

Hapa "homeri moja ya shayiri huwakilisha kipande cha ardhi ambaho kingehitaji homeri moja ya shaiyiri ili kupandwa chote. : "kipanda cha ardhi kinachohitaji kudhamanishwa kwa homeri moja ya shayiri ili kuweza kupandwa chote" au " Thamani ya ardhiinayohitaji homeri moja ya shayiri itatakiwa"

homeri

homeri moja ni lita 220

shekeli hamsini za fedha

"vipande hamsini vya fedha , ambavyo kila kimoja bgramu kumi" au " gramu mia tano za fedha"

Leviticus 27:17

mwaka wa Yubile

Tazama maelezo ya sura 25:10

tathmini yake ya awali itabaki kuwa ileile

au "thamani yake itakuwa bei kamili

thamani yake lazima ishushwe.

"itamlazimu kupunguza thamani iliyokadiliwa"

Leviticus 27:19

haliwezi kukombolewa tena

Hii yaweza kumtakwa katika mtindo wa utendaji. : "hawezi kulirejesha kwa kulinunua tena"

Iwapo halikomboi shamba

Ule muda wa kukomboa shamba waweza kutamkwa wazi. : kama halikomboi shamba kabla ya mwak wa Yubile"

katika mwaka wa Yubile

AngTazama amaelezo ya sura ya 25:13

shamba lililotolewa kabisa kwa Yahweh

Hii yaweza kumtakwa katika mtindo wa utendaji. : "ambalo mtumwingie kalitoa kabisakabisa kwa Yahweh"

Leviticus 27:22

tenga

Ule msemo "tenga" humaanisha kutengwa kutoka kwenye kitu fula ili kutimiza kusudi fulani. . Waisraeli walitengwa kawa ajili ya huduma kwa Mungu. . Roho Mtakatifu aliwaagiza Wakristo huko Antiokia kuwatenga Paulo na Barnaba kwa kazi ambayo Mungu aliwataka wao waifanye . Mwamini "aliyetengwa" kwa ajili ya huduma kwa Mungu "kwakifishwa" kutimiza mapenzi ya Mungu. . maana mojawapo ya msemo "mtkatifu" ni kutengwa kuwa Mungu na kuwa umetengwa kutokanjia za dhambi za ulimwengu. . Ule msemo "takasa" humaanisha kutenga mtu kwa ajili ya huduma ya Mungu.

Leviticus 27:24

mtu yule ambaye lilikuwa limenunuliwa ... mmiliki wa ardhi

Virai hivi viwili humrejelea mtu yule yule. Kwa kawaida ardhi ingenunuliwa kutoka kwa mmiliki wake.

mtu yule ambaye lilikuwa limenunuliwa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "mtu aliyeliuza"

Tathmani yote lazima ifanywe

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "kuahani ataamua ukadiliaji wa thamani"

kwa uzani wa shekeli ya mahali pa patakatifu

Kulikuwa na shekeli za vipimo mbali mbali. Hiki kilikuwa ni kimojawapo ambacho watu ilikuwa watumie ndani ya hema takatifu.

Gera ishirini kwa shekeli moja.

Kusudi la sentensi hii ni kutamka ni kiasi gani shekeli ya patakatifu hupimwa. Gera ilikuwa ni uzani mdogo sana wa kipimo walichotumia Waisraeli: "Sharti shekeli moja iwe sawasawa na gera ishirini"

Gera ishirini kwa shekeli moja.

: "Shekeli moja yapasa ipime gramu kumi"

Leviticus 27:26

Asiwepo mtu atakayetenga

Hakuna awezaye kutenga kwa ajili ya Yahweh"

sehemu ya tano lazima itaongezwa kwenye thamani hiyo

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "naye atalzaimika kuongeza moja ya taon kwenye thamani hiyo"

Na kama mnyama hakombolewi

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Kama mtu hamtejeshi kwa kumnunua tena huyo mnyama"

naye atauzwa kwa thamani iliyowe

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji : "kuhani atamuuza kwa thamani iliyowekwa"

Leviticus 27:28

Hakutakuwa na kitu amabacho mtu anakitoa kwa Yahweh, kutoka katika vyote alivyonavyo, iwe ni mwanadamu au mnyama, au ardhi ya familia yake, ambacho chaweza kuuzwa au kukombolewa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Hukuna wawezaye kuuza au kukomboa kitu chochote mtu alichokitoa kwa Yahweh, kutoka katika vyote alivyonavyo, ama awe ni mwanadamu, mnyama, au ardhi ya familia yake", au "iwapo mtu amatoa kwa Yahweh kitu chochote alichonacho, ama awe mwanadamu au mnyama, au ardhi ya familia yake, hatakuwapo mtu anaweza kukiuza au kukikomboa"

Kila kitu kitolewacho ni kitakatifu sana kwa Yahwe

"Kila kitu mtu akitoacho ni kitakatifu sana kwa Yahweh"

Hakuna fidia inayoweza kulipwa

"hakuana akuwezaye kulipa fidia"

kwa kuwa mtu aliyelitolewa kwa ajili ya uangamizwa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "kwa kuwa mtu yeyote ambaye Yahweh kamtoa kwa ajili ya uangamivu"

Mtu huyo lazima auawe

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "lazima mmuue mtu huyo" au "yawapasa kumuua mtu"

Leviticus 27:30

Iwapo mtu anakomboa chochote cha zaka yake

Kama mtu anataka kurejesha tena zaka yake kwa kuinunua"

Leviticus 27:32

yeyote anayepita chini ya fimbo ya mchungaji

Hii hurejea njia ambayo wangehesabu wanyama wao. : "unapohesabu wanyama wwako kwa kuinua fimbo ya mchungaji wako na huku wakipita chini ya fimbo hiyo kwenda upande mwingine" au "munapowahesabu wanyama"

wa kumi mmoja lazima atengwe kwa ajili ya Yahweh

wakumi lazima atengwe kwa ajili ya Yahweh - sentensi yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "yawapasa mumtenge wa kumi mmoja kwa ajili ya Yahweh"

mmoja wa kumi

ya kumi- "kila mnyama wa kumi"

kisha wote wawili yule wa kwanza na huyo aliyebadiliwa

"kisha wanya wote wawili"

hawezi kukombolewa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Hataweza kumkomboa" au "Hataweza kummrejesha kwa kumnunutena"

Leviticus 27:34

Hizi ndizo amri

Huu ndiyo Mhitasari wa maelezo. Hurejerea zile amri zilizotolewa kwenye sura zilizotangulia.