Kiswahili: translationNotes Print

Updated ? hours ago # views See on WACS

1 Samuel 1

1 Samuel 1:1

Rama Msufi

Hili ni jina la kijiji kidogo kilichokuwa kilometa nane mashariki mwa Yerusalemu.

Elikana ... Yerohamu ... Elihu ... Tohu ... Sufu

Haya ni majina ya wanaume.

Penina

Hili ni jina la mwanamke.

1 Samuel 1:3

Mtu huyu

"Mtu huyu" inamuelezea Elikana.

Eli, Hofni na Finehasi

Haya ni majina ya wanaume.

1 Samuel 1:5

Hana

Hili ni jina la mwanamke.

Hasimu wake alimchokoza sana.

Mke mwingine alimdhihaki na kumuaibisha Hana.

Amelifunga tumbo lake

"amemfanya kuwa mgumba" au "amezuia kupata mimba."

1 Samuel 1:7

Hasimu wake

Huyu ni Penina mke mwingine wa Elikana. Hasimu ni mtu anayeshindana na mtu mwingine. Penina alikuwa anashindana na Hana na kujaribu kumfanya Elikana ampende yeye zaidi.

"Hana, kwa nini unalia? Kwa nini huli chakula? Kwa nini una huzuni moyoni mwako? Mimi si bora kwako kuliko wana kumi?

Swahi hili linaweza kutafsiriwa kama sentensi isemayo, "Hana usilie. Yakupasa ule na moyo wako ufurahi kwa sababu mimi ni bora kuliko wana kumi!"

Kuliko wana kumi

Elikana alitumia maneno haya kusisitiza kouonesha ni kwa kiasi gani Hana alikuwa na umuhimu kwake.

1 Samuel 1:9

Maelezo ya jumla:

Hana anaanza kuomba kwa Bwana na Eli anamtazama.

Hana alinyanyuka

Taarifa hii yaweza kuwa na maana ya kuwa Hema ya Hana ilikuwa karibu na maskani au alitembea toka kwenye Hema yake mpaka maskani kuomba. "Hana alinyanyuka na akaenda kwenye nyumba ya Bwana kuomba."

Wakati huo Eli kuhani

Hapa mwandishi anatuambia kuhusu mtu mwingine katika simulizi. Mtu huyu ni kuhani Eli.

Hekalu la Bwana.

Hekalu ni Hema lakini ilikuwa ni sehemu ambayo watu hutumia kuabudu hivyo ni vyema kuitafsiri kama Hekalu.

Alikuwa na uchungu sana.

Alikuwa ana katika matatizo makubwa au katika kuomboleza kwa sababu ya kutokuwa na mtoto na kuonewa na Penina mke mwingine wa Elikana.

1 Samuel 1:11

Taarifa ya jumla:

Maombi ya Hana kwa Bwana yanaendelea.

teso la mjakazi wako

Hii yaweza kuwa na maana ya 1) Hana kutokuwa na uwezo wa kuwa mjamzito au 2) namna ambavyo Penina anamdhihaki.

Unikumbuke

Hili ni ombi maalumu kwa Mungu. Mungu anajua yanayompata Hana hajasahau.

Usimsahau mjakazi wako

Hii ina maana sawa na "unikumbuke."

1 Samuel 1:12

Eli alimtazama

Eli alikuwa kuhani mkuu, hivyo alikuwa ndani ya hema ya Mungu na akiwaongoza.

1 Samuel 1:15

mimi ni mwanamke mwenye roho ya huzuni

"Mimi ni mwanamke mwenye huzuni sana"

nimemimina nafsi yangu mbele za Bwana

"Namwambia Bwana hisia zangu za ndani"

mjakazi wako

Hana anajizungumzia mwenyewe kwa kuonesha unyenyekevu.

nimekuwa nikiongea kutokana na maumivu na masikitiko yangu

Hii ni namna nyingine ya kusema kuwa ana "roho ya huzuni" Hii inaweza kutafsiriwa kama "Ninazungumza kwa sababu nina huzuni sana na hasimu wangu ananidhihaki sana"

maumivu na masikitiko

Maneno haya yote yanaonesha kuwa Hana amekosa raha na anahuzuni kwa sababu ya kudhihakiwa na Hasimu wake.

Maumivu

Haya ni mambo ambayo Penina alimfanyia ya kumuumiza.

Masikitiko

Hana anaelezea maumivu na aibu anayoipata kwa sababu ya namna Hana anavyomfanyia.

1 Samuel 1:17

Kisha Eli akamjibu

Eli akiliwa kuhani mkuu aliyeishi katika maskani.

Mjakazi wako

Hana anajizungumzia mwenyewe kwa kuonesha unyenyekevu na heshima kwa Eli kuhani mkuu.

na kula; uso wake

Hapa "uso wke" inamaanisha Hana mwenyewe.

1 Samuel 1:19

akamkumbuka

Mungu alijua yaliyokuwa yanampata Hana hakusahau.

Hana akapata mimba

"Hana akawa mjamzito?

1 Samuel 1:21

Nyumba yake

"Nyumba" inamaanisha watu wanaoishi ndani ya nyumba. "Familia yake"

Aache kunyonya

Kuacha kunywa maziwa na kuanza kula vyakula vyenye kimimimika.

ahudhurie mbele za BWANA na akae huko daima

Hana alimuahidi Mungu kuwa atamruhusu Samweli aishi na kufanyakazi na Eli katika hekalu.

kumnyonyesha mtoto

"kumpa mtoto wake maziwa"

1 Samuel 1:24

Efa

Efa ni kama lita 22 za unga.

Chupa

Mvinyo uliwekwa katika ngozi ya wanyama na sio chupa chuma.

1 Samuel 1:26

Akasema, "Ee bwana wangu! Kama uishivyo, bwana wangu

"Kama uishivyo" inaonesha kuwa Hana amekuwa mkweli na mwaminifu. "bwana ninachokwenda kukwambia ni kweli"

amenijibu ombi la dua yangu nililomwomba

Hana anazungumza juu ya dua kama kitu ambacho mtu anaweza kumpa mtu mwingine pia anazungumza juu ya dua kama jibu la ombi lake. Hii inaweza kutafsiriwa kama "amekubali kunifanyia nilichomuomba anifanyie"

Alimwabudu Bwana

Hii inamuelezea Elikana lakini tafsiri zingine humuelezea Elikana na familia yake.

nimempa BWANA

Hii inaweza kutafsiriwa kama "Nimemkopesha kwa Bwana"

1 Samuel 2

1 Samuel 2:1

Taarifa ya jumla:

Hana anamwimbia Bwana wimbo.

Moyo wangu wamtukuza

"nina furaha kubwa"

Katika Bwana.

"Kwa sababu ya Bwana" au "kwa sababu Bwana ni mkuu"

Pembe yangu imejulikana

Pembe ni ishara ya nguvu. "Sasa nina nguvu."

1 Samuel 2:2

Taarifa ya jumla:

Hana anaendelea kumwimbia Bwana.

hakuna mwamba kama Mungu wetu.

Hii ni namna nyingine ya kusema kuwa Mungu ni mwenye nguvu na mwaminifu.

Mwamba

Huu ni mwamba mkubwa ambao unaweza kujificha nyuma yake na kuwa juu ya adui.

1 Samuel 2:3

Taarifa ya jumla:

Hana anaendelea kumwimbia Bwana wimbo. Anazungumza kama vile watu wengine wanamsikiliza.

Hakuna majivuno

"hakuna maneno ya majivuno"

Kwa yeye matendo hupimwa

Hii inaweza kuandikwa kama "Yeye anapima matendo ya watu"

Pinde za mashujaa zimevunjika

Yaweza kuwa na maana ya 1) pinde zenyewe zimevunjika au 2) watu waliobeba pinde wamekatazwa kufanya. "Watu wenye ushujaa wamenyimwa kufanya"

Pinde za mashujaa zimevunjika

Hii inaweza kutafsiriwa kama "Bwana amezivunja pinde za mashujaa" au "Bwana amewafanya hata watu wenye nguvu kuwa dhaifu"

wale wanaojikwaa hujivika nguvu kama mshipi

Hii inamaanisha kuwa hawatajikwaa tena bali nguvu zao zitakuwa pamoja nao kama mshipi uliobana. "Bali atawafanya waliojikwaa kuwa na nguvu"

kujivika ... mshipi

Hiki ni kitendo cha kuvaa kitu kuzunguka kiuno na kujiandaa na kazi.

1 Samuel 2:5

Taarifa ya jumla:

Hana anaendelea kumwimbia Bwana.

amezaa saba

amezaa watoto saba

amenyong'onyea

kutokuwa na nguvu na kuwa mpweke.

1 Samuel 2:6

Taarifa ya jumla:

Hana anaendelea kumwimbia Bwana.

Bwana huua ... huuisha... hushusha... huleta juu ... humfanya mtu masikini ... mwingine tajiri ... hunyenyekeza ... hukweza.

Bwana ndiye mwenye mamlaka na kila kitu.

1 Samuel 2:8

Taarifa ya jumla:

Hana anaendelea kumwimbia Bwana.

Wahitaji

Watu wasiokuwa na kitu wanachohitaji.

toka mavumbini ... toka jalalani

Hii inaonesha hali ya watu wa daraja la chini katika jamii.

1 Samuel 2:9

Taarifa ya jumla:

Hana anaendelea kumwimbia Bwana.

anazilinda nyayo za watu wake waaminifu

"nyayo" inamaana ya njia za mtu anazopita, ambayo ni maisha ambayo mtu ameamua kuishi. "anawalinda watu wake waaminifu wasifanye maamuzi mabaya" au "anawasaidia watu wake waaminifu kufanya maamuzi ya busara"

waovu watanyamazishwa gizani

Hii ni njia ya busara ya kusemma kuwa Bwana atawaua watu waovu.

waovu watanyamazishwa

Neno "kunyamazishwa" inamaana ya "kumfanya anyamaze" Bwana atawafanya wanyamaze.

kwa nguvu

"kwa sababu ana nguvu"

1 Samuel 2:10

Taarifa ya jumla:

Hana anaendelea kumwimbia Bwana.

Wale wampingao BWANA watavunjwa

"Bwana atawavunja wale wanaompinga"

Kuvunjwa vipande vipanade

Hii inamaana ya "watashindwa"

miisho ya dunia

Neno hili linamaana ya kila sehemu. "dunia nzima"

kuinua pembe ya mtiwa mafuta wake

Pembe ni ishara ya nguvu. " viongozi aliowachagua atawapa nguvu zaidi ya adui zao"

mtiwa mafuta wake

Hii inaweza kutafsiriwa kama "aliyetiwa mafuta" Mafuta ilikuwa ishara kuwa Bwana amemchagua mtu huyo ambaye amempaka mafuta ili aongoze juu ya watu.

1 Samuel 2:12

Taarifa ya jumla:

Watu walipokuwa wakitoa dhabihu za wanyama, walichoma mafuta ya mnyama kwanza kisha walichemsha nyama na kula.

Hawakumjua Bwana

Hawakumsikiliza Bwana au kumtii.

Desturi

Desturi ni tendoambalo watu hulifanya mara kwa mara.

sufuria ... birika ... chombo ... chungu

Hivi ni vyombo vinavyotumika kupikia chakula.

sufuria

Ni chombo kidogo cha chuma kwa ajili ya kuchemshia.

Birika

Ni chombo kikubwa kizito cha chuma kwa ajili ya kuchemshia.

chombo

Ni chombo kikubwa kizito cha chuma kwa ajili ya kuchemshia.

chungu

Ni chombo cha udongo kwa ajili ya kupikia

1 Samuel 2:15

Taarifa ya jumla:

Watu walipokuwa wakitoa dhabihu za wanyama, walichoma mafuta ya mnyama kwanza kisha walichemsha nyama na kula.

mbaya, kabla

"Walifanya jambo bata zaidi kuliko hapo mwanzo."

Walichoma

"Mtu aliyetoa dhabihu alichukua dhabihu yake akaipeleka kwa kuhani kisha kuhani akaichoma"

Nipe nyama ya kuchoma kwa ajili ya kuhani

"Nipe mimi nyama ili nikampe kuhani aichome"

Kuchoma

Kupika juu ya moto

Kuchemsha

Kupika ndani ya maji

Mbichi

Haijapikwa

waliidharau dhabihu ya BWANA

Vijana hawakupenda maelekezo ya Bwana kuhusu dhabihu na hawakujali.

1 Samuel 2:20

sababu ya ahadi yake aliyoitoa kwa Bwana

Hana alimuomba Bwana ampe mtoto na aliahidi kuwa atamtoa mtoto amtumikie katika hekalu.

Mbele za Bwana

Mahali ambapo Bwana atamuona na Samweli atajifunza mambo ya Bwana.

1 Samuel 2:22

Kwa nini mnafanya mambo hayo?

Swali hili linaweza kutafsiriwa kama "Ni vibaya kufanya mambo haya!"

1 Samuel 2:25

ni nani atakayemtetea mtu huyo?

Swahi hili linaweza kiutafsiriwa kama sentensi "Hakuna mtu atakayemtetea mtu huyo."

kumtetea mtu huyo

"Kumuomba Bwana rehema juu ya mtu huyo"

Sauti ya baba yao

Sauti inawakilisha mtu. "Aliyoyasema baba yao"

1 Samuel 2:27

Mtu wa Mungu

Mara nyingi humaanisha nabii wa Bwana. "Mtu anayesikia na kusema maneno toka kwa Mungu"

Je, sikujifunua mwenyewe ... nyumba?

Swali hili linaweza kutafsiriwa kama sentensi "Mnapaswa kujua kuwa nilijifunua mwenyewe ... nyumba."

nyumba ya baba zako

"Nyumba" inamaanisha watu wanaokaa ndani ya nyumba. "Famila ya baba zako"

Baba yako

Haruni

apande madhabahuni kwangu, na kufukiza uvumba

Hii inamaana ya kutoa sadaka kwa Bwana.

kuvaa kanzu ya naivera mbele yangu

Maneno "kuvaa kanzu ya naivera" inaonesha kazi ya makuhani wanaovaa naivera. "Kufanya niliyowaamuru makuhani wafanye"

1 Samuel 2:29

Kwanini basi, unaidharau dhabihu yangu ... ninapoishi?

"Hampaswi kudharau dhabihu yangu ... mahali ninapoishi."

Mahali ninapoishi

"Mahali ambapo watu wangu huniletea dhabihu"

kujinenepesha ninyi wenyewe kwa uzuri wa kila sadaka

Sehemu nzuri ya sadaka ilitakiwa kuchomwa kama sadaka kwa Bwana lakini makuhali walikuwa wanakula.

Nyumba ya baba yako

"Nyumba" inamaanisha watu wanaokaa ndani ya nyumba. "Famila ya baba zako"

yawapasa kwenda mbele zangu

"Kuishi kwa kunitii mimi"

Mambo haya yapishe mbali nami nisifanye hivi

"Sitaruhusu familia yako wanitumikie daima"

wanaonidharau mimi hawatakuwa na thamani.

"Hawatakuwa na thamani hao wanaonidharau" au "Nitawadharau hao wanaonidharau"

1 Samuel 2:31

Tazama

"Sikiliza kwa makini ninayotaka kuzungumza" au "ninayotaka kuzungumza ni ya muhimu sana"

Nitaondoa nguvu zako na nguvu za nyumba za baba yako

"Nitakuua wewe pamoja na vijana wtote wenye nguvu wakiume wa uzao wa familia yako"

Nitasababisha macho yenu yashindwe

"nitasababisha mshinwe kuona" au "ntasababisha muwe vipofu"

1 Samuel 2:34

nitamwinua ... kuhani wangu mwaminifu

"Nitamfanya mtu awe kuhani"

kwa ajili yangu

"anitumikie mimi"

kile kilichomo moyoni mwangu na nafisini mwangu

"Ninachotaka afanye na nitakachomwambia afanye"

Nitamjengea nyumba madhubuti

Hapa "nyumba" imeelezewa kama "uzao." Nitahakikisha kuwa uzao wake unatumika kama kuhani mkuu.

1 Samuel 2:36

Yeye

Kuhani mwaminifu atakayeinuliwa na Bwana.

ili niweze kula kipande cha mkate

"Kipande cha mkate kimetumika kama "chakula." Ili niweze kula.

1 Samuel 3

1 Samuel 3:1

Neno la Bwana halikupatikana kwa wimngi

"Bwana hakuzungumza mara kwa mara na watu"

Taa ya Mungu

Huu ni mshumaa wa saba uliopo mahali patakatifu pa maskani unaowaka kila siku mchana na usiku mpaka unapokwisha.

Hekalu la Bwana.

Hekalu ni Hema lakini ilikuwa ni sehemu ambayo watu hutumia kuabudu hivyo ni vyema kuitafsiri kama Hekalu.

1 Samuel 3:5

Mwanangu

Eli hakuwa baba yake na Samweli. Eli anazungumza kama vile yeye ndiye baba yake na Samweli kuonesha kuwa hajamkasirikia lakini Samweli anapaswa kumsikiliza.

1 Samuel 3:7

wala hakuwahi kupata ujumbe wowote kutoka kwa BWANA ukifunuliwa kwake

"Wala Bwana hakukufunua ujumbe wowote kwake"

1 Samuel 3:9

Mtumishi wako ana

Eli alimwambia Samweli azungumze na Bwana ili Samweli aoneshe heshima kwa Bwana.

1 Samuel 3:10

Bwana alikuja na kusimama

Hii inaweza kuwa na maana ya 1) Bwana alimtokea Samweli na kusimama mbele yake au 2) Bwana alifanya uwepo wake uonekane kwa Samweli.

Mtumishi wako ana

Samweli anazungumza na Bwana na kuonesha heshima.

ambalo masikio ya kila mmoja yakisikia yatashtuka

Hapa "masikio ... yatashtuka" inamaanisha kuwa kila mtu atashituka kutokana na kitu atakachokisikia.

Kushtuka

Kuhisi kama vile mtu anakuchoma na kitu chenye ncha au kushtuka kwa sababu mtu amepiga kibao sehemu fulani ya mwili.

1 Samuel 3:12

kutoka mwanzo hadi mwisho

"karibu kila kitu"

walijiletea laana juu yao wenyewe

"walifanya mambo ambayo Bwana alisema kuwa atawaadhibu wanaofanya mambo hayo"

dhambi za nyumba yake hazitasahehewa kwa dhabihu au kwa sadaka

"Hakuna dhabihu au sadaka ambayo mtu ataitoa na kufanya dhambi za nyumba hii zisamehewe"

Dhambi za nyumba yake

"dhambi ambazo watu wa nyumba yake wamefanya"

1 Samuel 3:15

Nyumba ya Bwana

"nyumba" ni hema lakini hapa imetafsiriwa kama nyumba.

Mwanangu

Eli hakuwa baba yake na Samweli. Eli anazungumza kama vile yeye ndiye baba yake na Samweli kuonesha kuwa hajamkasirikia lakini Samweli anapaswa kumsikiliza.

1 Samuel 3:17

Neno alilosema

"ujumbe alioutoa Bwana"

Mungu akutendee hivyo na kukuzidishia

Hii inaonesha ni kwa namna gani Eli alikuwa anasisitiza "Mungu akuadhibu sawasawa na alivyosema ataniadhibu na hata zaidi"

1 Samuel 3:19

hakuacha kutimiza maneno yake ya unabii

"alifanya mambo yote aliyoyafanyia unabii kutimia"

Israeli yote

Watu wote wa Israeli.

tokea Dani hadi Beersheba

"sehemu zote za nchi" au "toka mwisho wa nchi hadi upande mwingine"

Samweli aliteuliwa

Bwana alimteua

1 Samuel 4

1 Samuel 4:1

Ebenezeri ... Afeki

Haya ni majina ya mahali.

Israeli ilishindwa na Wafilisti

"Wafilisti waliwashinda Waisraeli na kuwaua."

watu wapatao elfu nne

Idadi hii sio kamili yaweza kuwa zaidi ya watu elfu nne au pungufu ya watu elfu nne, hii inaonesha kuwa hakukuwa na idadi kamili.

1 Samuel 4:3

Watu

Askari waliokuwa wakipigani vitani.

Kwa nini BWANA ametushinda leo mbele ya Wafilisti? Hebu tulilete

Wazee hawakujua kwa nini Bwana amewashinda lakini walifikiri kuwa wanafahamu namna ya kufanya ili hali hiyo isijirudie tena.

akaaye juu ya makerubi

Japokuwa Bwana yupo kila mahali alijionesha mwenyewe kwa wana wa Israeli juu ya makerubi waliokuwepo juu ya sanduku.

Finehasi

Finehasi huyu hakuwa mjukuu wa Haruni katika Kutoka na Hesabu.

Walikuwepo huko

Walikuwepo Shilo.

1 Samuel 4:5

Sanduku la agano lilipokuja kambini

"watu walipolipeleka sanduku la agano la Bwana katika kambi" "Watu waliokuwepo pamoja na Hofini na Finehasi walilibeba sanduku la agano la Bwana na kulipeleka kambini."

Sanduku la Bwana lilifika kambini

"Watu walilipeleka sanduku la Bwana kambini"

1 Samuel 4:7

Wakasema ... wakasema

Wafilisti walisemezana wao kwa wao. "walisemezana wao kwa wao... walisemezana wao kwa wao"

mungu ameingia

Wafilisti waliabudu miungu mingi hivyo waliamini kuwa moja kati ya miungu ambayo hawakuiabudu alikuja kambini. Walikuwa wakizungumza juu ya Mungu wa Israeli. Baadhi ya tafsiri zinasomeka "Mungu ameingia"

miungu yenye nguvu ... miungu inayoshambulia

Kwa sababu neno mungu (au Mungu) katika sura ya 4:7 ni umoja tafsiri nyingi zimeandika "mungu mwenye nguvu ... mungu anayeshambulia" au "Mungu mwenye nguvu ... Mungu anayeshambulia" tumia jina sahihi la Mungu wa Israeli.

Ni nani atatulinda dhidi ya nguvu za Mungu mwenye uwezo?

Swali hili linaonesha hisia za uoga. "Hakuna mtu atakayetulinda na Mungu huyu mwenye uwezo."

Kuweni wanaume

"kuweni na nguvu na mpigane"

1 Samuel 4:10

Israeli wakashindwa

"Waliwashinda Waisraeli" Hapa Israeli inamaanisha jeshi la Israeli.

Sanduku la Mungu lilichukuliwa

"Wafilisti walilichukua sanduku la Mungu.

1 Samuel 4:12

mavazi yamechanika na matope kichwani mwake

Hii ni njia ya kuonesha maombolezo makubwa katika desturi ya Israeli.

moyo wake ulitetemeka kwa ajili

Eli aliogopa kuwa jambo fulani baya limetokea.

Mji mzima

"Watu wote wa mji."

1 Samuel 4:14

Mtu

"Mtu wa Benyamini"

1 Samuel 4:16

Akamwambia

"Eli akasema"

Mwanangu

Eli hakuwa baba yake na Samweli. Eli anazungumza kama vile yeye ndiye baba yake na Samweli kuonesha kuwa hajamkasirikia lakini Samweli anapaswa kumsikiliza.

Israeli wamewakimbia Wafilisti

Hii inaelezea juu ya kilichotokea.

Pia kumekuwa ... watu. Pia watoto wako wawili

"Sasa nitakwambia kitu kibaya ... sasa nitakwambia kitu kibaya" au "Sio hayo tuu yaliyotokea huko ... lakini watoto wako wawili"

Sanduku la Bwana limechukuliwa

"Wafilisti wamechukua sanduku la Bwana"

1 Samuel 4:18

Alipotamka

"Yule mtu wa Benyamini alipotamka"

Kutamka

"Kuzungumza"

Shingo yake ilivunjika

"Shingo yake ilivunjika kwa sababu alianguka"

1 Samuel 4:19

Mkwe wake

"mkwe wa Eli"

Sanduku la Bwana limekamatwa

"Wafilisti wamelikamata sanduku la Bwana"

Aliyaweka moyoni yale aliyoambiwa

"aliyazingatia yale aliyoambiwa"

1 Samuel 4:21

Ikabodi

Jina hili lina maana ya "hakuna utukufu"

Kwa sababu sanduku la Mungu limetekwa nyara ... sababu sanduku la Mungu limetekwa nyala.

"Kwa sababu Wafilisti wameteka nyara sanduku la Mungu ... Kwa sababu Wafilisti wameteka nyara sanduku la Mungu"

1 Samuel 5

1 Samuel 5:1

Basi

Neno hili linaonesha mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

Nyumba ya Dagoni

Hili ni hekalu la Dagoni mungu wa Wafilisti.

Tazama Dagoni

"Walipatwa na mshangao walipoona Dagoni"

Dagoni ilianguka chini kifudifudi

Msomaji anatakiwa atambue kuwa Bwana alisababisha sanamu ianguke chini wakati wa usiku.

1 Samuel 5:4

Dagoni alikuwa ameanguka

Msomaji anatakiwa atambue kuwa Bwana alisababisha Dagoni aanguke.

Kichwa cha Dagoni na vitanga vyake viwili vilikatika na kulala

Ilikuwa kama vile Bwana ni askarialiyewashinda adui zake na kuwakata kichwa na mikono.

Mikono

Vitanga vya mikono vimanaanisha mikono yote.

Na hii ndiyo sababu, hata leo

Mwandishi anatuelezea taarifa na kutenganisha na simulizi inayosimuliwa.

1 Samuel 5:6

Mkono wa Bwana ulikuwa mzito juu ya

"Bwana aliwahukumu sana"

majipu

Huu ni ugonjwa wa ngozi.

Ashdodi na wilaya zake kwa pamoja

"Watu wote wa Ashdodi na watu wa nchi inayozunguka Ashidodi"

walipotambua

"walipofahamu"

sanduku la Mungu wa Israeli

Yaweza kuwa na maana ya 1) walikuwa wakizungumza juu ya jina kamili la Mungu wa Israeli au 2) waliamini kuwa Israeli waliabudu moja kati ya miungu mingi.

1 Samuel 5:8

wafanye juu ya sanduku la Munga wa Israeli ... Sanduku la Mungu wa Israeli lihamishwe

Yaweza kuwa na maana ya 1) walikuwa wakizungumza juu ya jina kamili la Mungu wa Israeli au 2) waliamini kuwa Israeli waliabudu moja kati ya miungu mingi.

Wakalibeba sanduku la Mungu wa Israeli.

Mwandishi anatumia jina sahihi la Mungu wa Israeli.

Mkono wa Bwana ulikuwa dhidi ya

"Bwana aliadhibu"

wote wakubwa kwa wadogo

Wao wote "wadogo kwa wakubwa, masikini na tajiri"

Majipu

Huu ni ugonjwa wa ngozi.

1 Samuel 5:10

Walipiga kelele

"walipiga kelele kwa hofu"

1 Samuel 5:11

Mungu wa Israeli

Yaweza kuwa na maana ya 1) walikuwa wakizungumza juu ya jina kamili la Mungu wa Israeli au 2) waliamini kuwa Israeli waliabudu moja kati ya miungu mingi.

kulikuwa na hofu ya kutisha mjini mwote

Watu wote wa mji waliogopa kuwa watakufa"

Mkono wa Mungu ulikuwa mzito mno huko

"Mungu aliwaadhibu sana watu huko"

Watu ambao hawakufa

Hii inaonesha kuwa watu wengi walikufa.

Majipu

Huu ni ugonjwa wa ngozi

kilio cha mji kilipanda hadi mbinguni

"Watu wa mji walilia kwa sauti kubwa" Neno "mbinguni" linamaanisha miungu ya watu. "Watu wa mji wakaililia miungu yao"

1 Samuel 6

1 Samuel 6:1

Makuhani na waganga

Hawa walikuwa ni makuhani na waganga wa kipagani walimwabudu Dagoni.

wambieni jinsi ambavyo tunapaswa kulirudisha

Wafilisti walitaka kujua namna watakavyolirudisha sanduku la Bwana bila kumkasirisha zaidi.

1 Samuel 6:3

Mungu wa Israeli

Yaweza kuwa na maana ya 1) walikuwa wakizungumza juu ya jina kamili la Mungu wa Israeli au 2) waliamini kuwa Israeli waliabudu moja kati ya miungu mingi.

kwa namna yoyote ile mpelekeeni sadakaa ya hatia

Maneno "kwa namna yoyote ile" ni namna ya kuelezea jamno. "Lazima mpeleke sadaka ya hatia"

Mtapona

"hamtaumwa tena"

Ninyi

Ni wingi inayomaanisha Wafilisti wote.

kwa nini mkono wake hadi sasa haujaondoka juu yenu

"Mkono" imetumika kuwakilisha nguvu za Mungu za kuadabisha. "kwa nini hajayaondoa mateso yenu"

Majipu

Huu ni ugonjwa wa ngozi.

Panya

Hapa anaelezea panya zaidi ya mmoja.

1 Samuel 6:5

Mifano

Mifano ni kitu kinachofanana na kitu fulani.

Majipu

Ni ugonjwa wa ngozi.

Panya

Hapa anaelezea panya zaidi ya mmoja.

ambayo huiharibu

"ambayo huangamiza"

Mungu wa Israeli

Yaweza kuwa na maana ya 1) walikuwa wakizungumza juu ya jina kamili la Mungu wa Israeli au 2) waliamini kuwa Israeli waliabudu moja kati ya miungu mingi.

ataondoa mkono wake kutoka juu yenu, kutoka juu ya miungu yenu, na kutoka juu ya nchi yenu.

ataondoa mkono wake kutoka juu yenu, kutoka juu ya miungu yenu, na kutoka juu ya nchi yenu. "ataacha kuwaadhibu ninyi na miungu yenu na nchi yenu."

Kwanini mfanye mioyo yenu kwa migumu, kama vile Wamisri na Farao walifanya mioyo yao kuwa migumu?

Makuhani na waganya wanatumia swali ili kuwafanya Wafilisti wafikirie kwa makini juu ya kile kitakachowapata ikiwa watakataa kumtii Mungu.

Kuifanya mioyo yenu kuwa migumu.

"kuacha kumtii Mungu"

Je, Wamisri hawakuwaachilia watu, na wakaondoka?

Hili swali limetumika kuwakumbusha Wafilisti kuwa Wamisri waliwaruhusu Waisraeli watoke Misri ili Mungu aache kuwaadhibu Wamisri.

1 Samuel 6:7

Ng'ombe wawili wanyonyeshao

"Ng'ombe wawili wenye ndama ambao bado wananyonya"

Ndipo mlipeleke lipate kuondoka.

Ng'ombe wawili watakwenda nyumbani kwenye ndama wao.

ikiwa watakwenda ... hadi Beth Shemeshi, basi mjue kuwa ni Bwana

Sio kawaida kwa ng'ombe kuchagua kwenda Beth Shemeshi wakati ndama wamerudi kwenye nchi ya Wafilisti.

1 Samuel 6:10

Ng'ombe wawili wanyonyeshao

"Ng'ombe wawili wenye ndama ambao bado wananyonya"

Mumbo ya majipu yao

"Mfano wa majipu yao"

Majipu

Huuu ni ugonjwa wa ngozi.

Ng'ombe waliondoka moja kwa moja kuelekea Beth Shemeshi

Ng'ombe wanaonyonyesha huwarudia ndama wao lakini ng'ombe hawa walikwenda Beth Shemeshi.

Wakipiga kelele walipokuwa wakienda

Kupiga kelele ni milio waliyokuwa wanatoa ngombe sauti zao.

hawakugeuka upande wa kushoto au kulia

"Walikwenda moja kwa moja mbele"

1 Samuel 6:13

Basi

Mwandishi anatambulisha sehemu mpya ya simulizi.

watu wa Beth Shemeshi

Hawa walikuwa Waisraeli.

Waliponyanyua macho yao

Walipotizama juu

1 Samuel 6:14

Kulikuapo jiwe kubwa mahali hapo

Jiwe hili ndilo jiwe lililotumika kama madhabahu walipotoa sadaka ya ng'ombe kama dhabihu.

Walawi walilitelemsha chini sanduku la Bwana

Hii ilitokea baada ya kutayarisha kuni zilizotokana na mkokoteni na kutengeneza moto uliotumika kutolea sadaka ya ng'ombe kwa Bwana.

Walawi walilitelemsha chini sanduku

Kutokana na sheria za Musa Walawi tuu ndio walioruhusiwa kulishughulikia sanduku.

pamoja na kasha lake lililoyatunza yale maumbo ya dhahabu,

"kasha ambalo maumbo ya dhahabu ya panya na majipu yalikuwepo"

1 Samuel 6:16

Viongozi watano wa Wafilisti

"Wafalme watano wa Wafilisti"

1 Samuel 6:17

Majipu

Huu ni ugonjwa wa ngozi

Panya

Hapa ana maana ya panya zaidi ya mmoja.

miji iliyojengewa maboma

Hii ni miji iliyozungushiwa kuta ndefu ili kuwalinda watu waliopo ndani yake wasivamiwe na adui.

Lile jiwe kubwa ... likabaki kama ushuhuda

Jiwe linafananishwa kama mtu awezaye kuona. "Jiwe kubwa ... bado liko hapo na watu wanakumbuka yaliyotokea juu yake"

Yoshua Mbeth- Shemeshi

"Yoshua toka Beth- Shemeshi"

Hadi leo

Hata wakati ambao mwandishi aliandika kitabu.

1 Samuel 6:19

walichungulia ndani ya sanduku

Sanduku lilikuwa takatifu sana na hakuna mtu aliyeruhusiwa kulitizama nadani. Makuhani tuu ndio walioruhusiwa.

Aliwaua watu sabini

"Aliwaua watu 70"

Je, ni nani awezaye kusimama mbele ya BWANA, huyu Mungu mtakatifu?

Yaweza kuwa na maana ya 1) Hakuna mtu anayeweza kushindana na Bwana kwa sababu ni mtakatifu. au 2) Yatupasa kumtafuta mtu atakayemtumikia Bwana kama Kuhani, je nani kati yetu anastahili?

Atapanda kwenda kwa nani kutoka kwetu?

Hili ni swali ambalo watu wanatafuta majibu. Yaweza kuwa na maana ya 1) "Bwana atakwenda kwa nani kutoka kwetu?" au 2) "sanduku litakwenda kwa nani kutoka kwetu?"

1 Samuel 6:21

Kiriath Yearimu

Huu ulikuwa mji katika Israeli.

1 Samuel 7

1 Samuel 7:1

Kiriath Yearimu

Hili ni jina la mahali.

Abinadabu ... Eleazari

Haya ni majina ya wanaume.

Miaka ishirini

"Miaka 20"

1 Samuel 7:3

Nyumba yote ya Israeli

"Nyumba" inamaanisha watu wanaoishi ndani ya nyumba na uzao wao. "Uzao wote wa Israeli" au "watu wote wa Israeli"

Kumrudia Bwana kwa moyo wenu wote

"Kujitoa moja kwa moja kumuabudu na kumtii Bwana tuu"

1 Samuel 7:5

Israeli wote

"Watu wote wa Israeli" au "Waisraeli wote"

Kumwaga chini mbele za Bwana

Hii yaweza kuwa na maana ya 1) watu walijinyima maji kama sehemu ya kufunga au 2) walitoa maji visimaji na kuyamwaga chini kama ishara ya kuonesha namna gani wanajutia dhambi zao.

1 Samuel 7:7

viongozi wa Wafilisti waliwashambulia Israeli

"Viongozi wa Israeli waliongoza majeshi yao kuishambulia Israeli"

atuokoe kutoka mkono wa Wafilisti

"atuokoe toka kwenye jeshi la Wafilisti"

1 Samuel 7:9

ndama mchanga

Ndama ambaye bado ananyonya maziwa ya mama yake.

Akamlilia

Akaomba msaada

Bwana akamjibu

Bwana akafanya yale ambayo Samweli alimuomba ayafanye.

1 Samuel 7:10

Hata Samweli ... Beth kari

Hii inaelezea kuwa mwandishi anamaanisha kuwa "Bwana alimjibu"

Kuwachanganya

Kusababisha Wafilisti washindwe kufikiri vizuri na wasijue la kufanya.

Wakashindwa mbele ya Israeli

Hii inaweza kutafsiriwa kama 1) Bwana akawafanya washindwe mbele ya Israeli" au "Israeli wakawashinda wao."

Kuwashindwa

Kuwashinda watu ni kuwadhibiti kabla hawasababisha maafa.

Beth kari

Hili ni jina la mji.

1 Samuel 7:12

Akachukua jiwe na kulisimamisha

Waisraeli na watu wengine wa nchi ile waliweka jiwe kubwa mahali ambapo matukio ya muhimu yalitokea kama kumbukumbu ya msaada wa Mungu.

Mispa ... Sheni

Haya ni majina ya mahali.

1 Samuel 7:13

Kwa hiyo, Wafilisti walishindwa

Mwandishi anamaliza kuwa kutuelezea namna ambavyo Wafilisti walishindwa.

Wafilisti walishindwa

Bwana aliwafanya Wafilisti washindwe.

hawakuingia katika mipaka ya Israeli

Wafilisti hawakuingia katika mpaka wa Israeli ili kuwashambulia.

Mkono wa Bwana ulikuwa dhidi ya Wafilisti.

"Bwana alitumia nguvu zake dhidi ya Wafilisti"

Miji ... kutoka kwa Israeli ikarudishwa kwa Israeli

Hii inaweza kuwa na maana ya 1) "Bwana aliirudisha miji ya nchi ya Israeli ... toka Israeli" au 2) "watu wa Israeli waliweza kuidai miji yao ... toka Israeli"

1 Samuel 7:15

Wakazunguka

Wakasafiri toka sehemu moja mpaka nyingine kwa kuzunguka.

Aliamua migogoro

Migogoro ni malumbano au kutokuelewana kati ya watu wawili au zaidi.

1 Samuel 8

1 Samuel 8:1

walipiga mbio kutafuta mapato ya udhalimu

"Walifanya kazi kwa nguvu ili kupata mapato kwa njia ya udhalimu"

Kupotosha hukumu

"Kutoa hukumu kwa kuwapendelea wanaofanya uovu"

1 Samuel 8:4

hawaenendi katika njia zako

"hawafanyi vitu unavyofanya" au "hawafanyi kama vile unavyofanya wewe"

Tuchagulie mfalme wakutuamua kama yalivyo mataifa yote

Hii yaweza kuwa na maana ya 1) "Tuchagulie mfalme kama wafalme wa mataifa yote ili atuamue" au Tuchagulie mfalme atakayetuamua kama wafalme wa mataifa wanavyowaamua wao"

Tuchagulie mfalme wakutuamua

Viongozi waliamini vibaya kuwa mfalme na wana wake wataongoza kwa haki.

1 Samuel 8:6

Lakini haikumpendeza Sameli ... Utupatie mfalme

Samweli hakuwa na furaha kwamba watu hawakutaka yeye awaondoe watoto wake waliokuwa waovu na kumteua mwamuzi mwingine lakini walitaka mfalme wa kutawala juu yao kama nchi nyingine zinavyofanya.

Sikiliza sauti ya watu

Hapa neno "sauti" linamaana ya mapenzi au matakwa ya watu. "Fanya kama vile watu wanavyotaka"

bali wamenikataa mimi

Bwana alijua kuwa watu hawakuwakataa viongozi waovu tuu bali walimkataa yeye kama mfalme wao.

1 Samuel 8:8

Niliwatoa Misrai

Hiki ni kitendo cha Bwana kuwatoa Waisraeli utumwani Misri miaka mingi iliyopita.

Sasa wasikilize

"Sasa fanya kama vile wanavyokuomba ufanye"

Waonye sawasawa

"uwe makini unapowaonya"

1 Samuel 8:10

Hivi ndivyo mfalme atakavyotawala ... atachukua

Matendo ya mfalme yatakuwa kuchukua. Huu ni mwanzo wa vitu ambavyo mfalme atachukua.

Hivi ndivyo jinsi mfalme atakavyowatawala.

"Hivi ndivyo mfalme atakayetawala juu yenu atakavyofanya"

Atawaweka juu ya magari yake

"Atawafanya waendeshe magari vitani"

Kuwa wapanda farasi wake

Wataendesha farasi kwenda vitani.

1 Samuel 8:13

Taarifa ya jumla:

Samweli anaendelea kuwaambia vitu ambavyo mfalme atavichukua.

kuwa watengeneza manukato

"Kutengeneza mafuta yanayonukia vizuri kwa ajili ya kujipaka mwilini"

mizeituni

"mashamba ya miti ya mizeituni"

moja ya kumi ya nafaka zenu

Watagawanya nafaka zao katika mafungu kumi yaliyosawa kisha kutoa fungu moja maafisa wa mfalme na watumishi.

moja ya kumi ya mizabibu

Watagawanya divai waliyoipata toka kwenye mizabibu katika mafungu kumi kisha kutoa fungu moja kwa maafisa wa mfalme na watumishi.

Afisa

Ni kiongozi katika jeshi la mfalme.

1 Samuel 8:16

Taarifa ya jumla:

Samweli anaendelea kuwaambia vitu ambavyo mfalme atavichukua.

moja ya kumi ya mifugo yenu

Watagawanya mifugo yao katika mafungu kumi yaliyosawa kisha kutoa fungu moja maafisa wa mfalme na watumishi.

mtakuwa watumwa wake

"mtahisi kama vile nyie ni watumwa wake"

Mtalia

Yaweza kuwa na maana ya 1)watu watamuomba Bwana awaokoe toka kwa mfalme au 2) watu watamuomba mfalme aache kuwanyanyasa.

1 Samuel 8:21

akayarudia katika masiko ya Bwana.

"Masikio ya Bwana" inamuelezea Bwana. Samweli alimuomba Bwana kwa kurudia yote ambayo watu walimwambia.

Sikiliza sauti yao

"Wasikilize watu"

uwafanyie mfalme

"Mfanye mtu kuwa mfalme juu yao"

arudi mjini kwake

"akarudi nyumbani"

1 Samuel 9

1 Samuel 9:1

Taarifa ya jumla

Mwandishi anatupa taarifa ya jumla katika mistari hii.

mtu mashuhuri

Mtu ambaye watu wanamuheshimu na wanasikiliza anachokisema.

Kishi ... Abieli ... Zerori ... Bekorathi ... Afia

Haya ni majina ya wanaume katika ukoo ya familia ya sauli.

Mbenyamini

Mbenyamini ni mtu anayetoka katika kabila la Wabenyamini.

mzuri wa uso

Mtu mwenye muonekano mzuri.

Kutoka mabegani kwenda juu alikuwa mrefu kuliko watu wengine

Watu wengine warefu katika Israeli hawakumfikia mabegani wake.

1 Samuel 9:3

Sasa

Mwandishi ameanza sehemu mpya ya simulizi.

amka

"acha kufanya unachokifanya"

nchi ya vilima vilima ya Efraimu ... nchi ya Shalisha ... nchi ya Shaalimu ... nchi ya Wabenyamini

Haya ni maeneo katika Israeli.

hawakuwaona ... hawakuwa huko ... hawakuwaona

Hapa wanazungumziwa punda.

1 Samuel 9:5

nchi ya Sufu

Hili ni eneo katika Israeli kaskazini mwa Yerusalemu.

Mtu wa Mungu

Mara nyingi humaanisha nabii wa Bwana. "Mtu anayesikia na kusema maneno toka kwa Mungu"

tupitie wapi katika safari yetu

"tupite njia gani ili tuwapate punda wetu"

1 Samuel 9:7

twaweza kumpelekea nini?

Kupeleka zawadi ni alama ya heshima kwa mtu wa Mungu.

Mtu wa Mungu

Mara nyingi humaanisha nabii wa Bwana. "Mtu anayesikia na kusema maneno toka kwa Mungu"

robo ya shekeli

Robo ya shekeli ni aina ya fedha ambayo ilitumika katika agano la kale.

1 Samuel 9:9

Zamani katika Israeli ... mwonaji

Hii ni taarifa ya desturi ambayo iliongezwa na mwandishi wa Kiebrania.

Kwa maana nabii wa leo, zamani aliitwa Mwonaji

"Mwonaji ni jina la zamani la nabii"

1 Samuel 9:12

leo watu wanatoa dhabihu

Hizi ni kama sikukuu au dhabihu za matunda ya kwanza, sio dhabihu za dhambi ambazo lazima zifanyikie katika hema.

1 Samuel 9:14

akipanda kwenda mahali pa juu

Hapa ni mahali ambapo watu wamepafanya kuwa mahali patakatifu pa kutolea dhabihu na sadaka kwa Bwana.

1 Samuel 9:15

Taarifa ya jumla:

Mwandishi ameacha kutuelezea simulizi na anatoa taarifa ya jumla ili msomaji aelewe ni kitu gani kinafuata.

nawe utamtia mafuta awe mkuu

Neno mkuu limetumika badala ya neno mfalme. Huyu ni mtu ambaye Bwana amemchagua awe mfalme wa Israeli.

nchi ya Benyamini

"nchi ambayo watu wa kabila la Benyamini waliishi"

kutoka kwenye mkono wa Wafilisti

"Ktutoka kwenye utawala wa Wafilisti"

Kwa kuwa nimewaonea huruma watu wangu

"Watu wangu wanateseka na ninataka kuwasaidia"

1 Samuel 9:17

Bwana akamwambia

"Bwana akamwambia Samweli"

Mwonaji

"Nabii wa Bwana"

1 Samuel 9:20

Na yote yaliyotamanika kwa ajili ya Israeli yanamwangukia nani? Siyo kwako na nyumba ya baba yako yote?

Maswali haya yanaelezea kwa undani kuthibitisha kuwa Sauli ndiye aliyechaguliwa na Bwana kuwa Mfalme wa Israeli.

Siyo mimi Mbenyamini ... ya Israeli? Kwa nini basi unaniambia kwa namna hii?

Sauli anashangaa kwa sababu Waisraeli wwengine walilichukulia kabila la Benyamini kama kabila ovu na Wabenyamini walichukulia ukoo aliotoka Sauli kuwa haukuwa wa muhimu.

1 Samuel 9:22

Ukumbini

Mwandishi anaonesha kuwa karibu na sehemu ya kutolea dhabihu kulikuwa na jengo kubwa ambalo watu walikuwa wakila pamoja huko.

mahali pa heshima

"Hiki ni kiti cha heshima"

thelathini

"30"

1 Samuel 9:23

paja lililokuwa limeinuliwa katika dhabihu

Kuhani aliyeinua paja katika dhabuhu ndiye anayepaswa kula. Samweli alimfanya Sauli ale ili kuonesha kuwa kuwa mfalme ni kazi takatifu.

Kilichokuwa pamoja nayo

Yaweza kuwa na maana ya 1)chakula kingine ambacho Sauli alikula pamoja na nyama au 2) sehemu nyingine ya ng'ombe.

Kisha Samweli akasema

Hii yaweza kuwa na maana ya "Mpishi akasema."

Na kwa sasa waweza kusema, 'Nimewaalika watu.'

Yaweza kuwa na maana ya 1) Sauli anaweza kusema kuwa aliwaalika watu au 2) Samweli aliwaalika watu

1 Samuel 9:25

darini

Hii ilikuwa sehemu ya kawaida kwa familia na wageni kula na kulala. Huwa na ubaridi jioni usiku kuliko sehemu nyingine za nyumba.

Samweli alimwita Sauli darini na kusema

"Sauli alipokuwa amelala darini Samweli alimuita na kusema"

1 Samuel 9:27

mbele yetu ... na alitangulia mbele ... Lakini wewe sharti usubiri

Yaweza kuwa na maana ya "mbele yetu na atakapokwenda mbele yetu yakupasa usubiri"

nipate kukuambia ujumbe wa Mungu

"Ili nikuambie ujumbe wa Mungu kwa ajili yako"

1 Samuel 10

1 Samuel 10:1

akachukua chupa ya mafuta, akayamimina juu ya kichwa cha Sauli

Katika tamaduni za Israeli nabii inapomimina mafuta katika kichwa cha mtu huyo mtu anapokea baraka toka kwa Bwana.

Chupa

Ni chombo kidogo kilichotengenezwa kwa udongo.

Je, Mungu hajakutia mafuta uwe mtawala juu ya urithi wake?

Samweli anajua jibu la swali hili. Anamkumbusha Sauli kuwa Bwana amemchagua yeye kuwa mfalme wa Israeli.

Selsa

Hili ni jina la mahali.

Nitafanya nini kuhusu mwanangu?

Baba yake na Sauli anaanza kuwa na hofu juu ya mtoto wake na anataka kumtafuta.

1 Samuel 10:3

Tabori

Hili ni jina la mahali.

kuchukua toka mikononi mwao

"kuchukua toka kwao" au "kukubali"

1 Samuel 10:5

Matari

Ni kifaa cha muziki kama ngoma ambacho kinaweza kupigwa na chenye vipande vya chupa huzunguka kifaa hicho, vipande hivi hulia kifaa kinapotikiswa.

Roho wa Bwana atakujaza

Hii inamaana kuwa roho wa Bwana atamchochea Sauli. Atamfanya Sauli atoe unabii na kuwa tofauti na watu wengine.

1 Samuel 10:7

fanya lolote ambalo mikono yako itaona ifanye

Hapa Samweli anazungumza juu ya mikono ya Sauli. "fanya kile ambacho unafikiri ni sahihi kufanya"

1 Samuel 10:9

Mungu akampa moyo mwingine

Mungu akamfanya Samweli afikiri tofauti na alivyofikiri mwanzo.

Roho ya Mungu ikamjilia

"Roho ya Mungu ikamtawala kabisa.

1 Samuel 10:11

Kitu gani kimempata mtoto wa Kishi?

Hii inaweza kuwa na maana ya 1) watu wanauliza ili kupata taarifa au 2) yaweza kuwa Swali linaloonesha kuwa Sauli sio wa muhimu. "Kishi sio mtu wa muhimu hivyo haiwezekani mtoto wake akawa nabii"

Mwana wa Kishi

"Sauli, mwana wa Kishi"

Na ni nani baba yao?

Swali hili linawakumbusha watu kuwa kuwa nabii haina uhusiano na baba yako ni nani. "Haijalishi Manabii hawa wazazi wao ni akina nani"

Kwa sababu ya jambo hili, ukawapo msemo, "Hivi Sauli naye ni mmoja wa manabii?"

"Na hii ndiyo sababu, wakati ambapo watu hawakuamini baadhi ya taarifa walifikiri juu ya kilichotokea kwa Sauli na kusema 'Hivi Sauli naye ni mmoja wa manabii?'"

Hivi Sauli naye ni mmoja wa manabii?

Kwa Sababu Sauli ni mmoja wa manabii watu walifikiri kuwa hata watu wasiokuwa na umuhimu wanaweza kuwa manabii.

1 Samuel 10:14

Ndipo baba yake mdogo na Sauli akamwambia

"Ndipo kaka yake na baba yake na Sauli akamwambia Sauli"

Hakumwambia kuhusu swala la ufalme

"Sauli hakumwambia baba yake mdogo kuwa Mungu amemchagua kuwa mfalme wa Israeli"

1 Samuel 10:17

Niliwatoa Israeli kutoka Misri

"Niliwatoa watu wa Israeli kutoka Misri"

Leo

"sasa"

Mkono wa Wamisri ... mkono wa falme zote

"Mkono" inamaanisha mguvu. "Nguvu za Wamisri ... nguvu za mataifa yote"

Tuwekee mfalme juu yetu

Tupe mfalme wa kutuongoza.

jihudhurisheni wenyewe mbele za BWANA kwa kabila na jamaa zenu

"Wakusanye makabila na jamaa na msimame mbele za Bwana"

1 Samuel 10:20

Kabila la Benyamini lilichaguliwa ... jamaa ya Wamatri ikachaguliwa ... Sauli mwana wa Kishi akachaguliwa

"Bwana alichagua kabila la Benyamini... Bwana alichagua jamaa ya Wamatri... Bwana alimchagua Sauli mwana wa Kishi"

1 Samuel 10:22

alikuwa mrefu kuliko watu wote kuanzia mabega yake kwenda juu

Watu wengine warefu katika Israeli hawakumfikia mabegani wake.

1 Samuel 10:25

desturi na sheria za ufalme

"Mambo ambayo mfalme atawalazimisha wayafanye na mambo yote ambayo mfalme anapaswa kuyafanya"

1 Samuel 10:26

wenye mioyo iliyoguswa na Mungu

Mungu anapougusa mioyo ya watu ina maana ya kuwa Mungu ameweka kitu kwenye mioyo yao na kuwafanya watende jambo fulani.

Huyu mtu atatuokoaje?

"mtu huyu hana nguvu za kutuokoa"

Walimdharau

"Hawakumpenda"

1 Samuel 11

1 Samuel 11:1

Nahashi

Alikwa Mwamoni, uzao wa Lutu.

Yabeshi Gileadi

Hili ni jina la mahali.

Niling'oa

"Nilikata"

Kuleta fedheha

"kuleta aibu"

1 Samuel 11:3

Siku saba

"Siku 7"

1 Samuel 11:4

Gibea

Hili ni jina la mahali.

1 Samuel 11:6

Roho ya Mungu ikamjia kwa nguvu

Roho ya Bwana ikamchochea Sauli. Ikamfanya Sauli asababishe watu wamuogope kwa kumuheshimu kama mfalme wao na kujiunga na jeshi lake.

asiyejitokeza akimfuata

Sauli aliwaita watu wote wa Israeli waende kupigana dhidi ya Nahashi na Waamoni.

Na hofu ya Bwana ikawaingia watu

Bwana akasababisha watu wamuogope na kumuheshimu Sauli kama mfalme wao.

Beseki

Hili ni jina la mji ulikokuwa karibu na Yabeshi Gileadi.

watu wa Israeli walikuwa mia tatu elfu, na watu wa Yuda elfu thelathini.

"Watu wa Israeli walikuwa 300,000 na watu wa yuda walikuwa 30,000"

1 Samuel 11:9

Wakawaambia wale wajumbe

Hapa anazungumziwa Samweli na Sauli.

wakati wa jua kali

"kabla ya mchana"

Yabeshi Gileadi ... Yabeshi

Haya ni majina ya mahali.

Nahashi

Hili ni jina la mfalme.

1 Samuel 11:11

wakati wa asubuhi

Mda huu ni kabla ya mapambazuko ambapo watu wengi kwenye kambi walikuwa bado wamelala.

1 Samuel 11:14

Wakamsimika Sauli kuwa mfalme mbele za Bwana

"Wakamsimika Sauli kuwa mfalme wakati Bwana anaangalia"

Na huko walitoa sadaka za amani mbele za Bwana

Sehemu ya huduma ya Samweli kwa Bwana ni kutoa dhabihu japokuwa hakutoka katika ukoo wa Haruni wala wa Lawi.

1 Samuel 12

1 Samuel 12:1

yupo hapa mfalme aliyeko mbele yenu ... nami nimekuwako mbele yenu

Sentensi hizi zinaonesha kuwa watu waliweza kuona maisha ambayo Sauli na Samweli waliishi. "Maisha ya mfalme yalionekana ... maisha yangu yalionekana"

1 Samuel 12:3

Mimi niko hapa , Nishuhudieni mbele za BWANA na mbele za mtiwa mafuta wake.

Samweli anawasihi watu waeleze ikiwa amefanya jambo lolote baya.

Nimechukua ng'ombe wa nani? Nimechukua punda wa nani?

Samweli anatumia maswali kuwakumbusha watu kuwa hakuwahi kuwaibia wanyama wao.

Ni nani nimemdhulumu?

Samweli anatumia swali hili kuonesha kuwa amekuwa mkweli wakati wote.

Nishuhudieni, nami nitawarudishia

"Ikiwa nimefanya mabaya yoyote semeni sasa na nitawalipa mnavyonidai."

1 Samuel 12:4

kutoka mkono wa mtu yeyote ... kwenye mkono wangu

Hii ni namna nzuri ya kusema kuwa hakuiba waka kutoa au kupokea rushwa.

1 Samuel 12:6

matendo yote ya haki ya BWANA

Samweli anawaonesha historia ya Bwana alivyokuwa anawatendea Waisraeli, namna ilivyojawa na mambo mema na kusudi.

1 Samuel 12:8

Yakobo ... Musa ... Haruni ... Sisera

Haya ni majina ya watu.

Hazori

Hili ni jina la mahali.

akawauza

Hii inaelezea namna ambavyo Mungu aliwatoa juu ya adui zao kama watumwa.

Kwenye mikono ya Sisera ... Wafilisti ... Mfalme wa Moabu

"kwenye nguvu za Sisera ... Wafilisti na mfalme wa Moabu"

1 Samuel 12:10

Wakamlilia Bwana

Hawa ni taifa la Israeli.

tumewatumikia Mabaali na Mashtorethi

Kumtumikia imetumika hapa kama kumwabudu, "waliabudu miungu ya uongo"

Mkono wa adui zako

"Nguvu au utawala wa adui zako"

Yerubu Baali

Hili ni jina la heshima na nguvu ya kupigana na Mungu wauongo.

Bwana akawatuma ... na akawapa ushindi

Samweli anasimulia simulizi ya namna ambavyo Mungu alifanya baada ya watu kutubu dhambi zao na kuomba msaada.

Yerubu Baali, Bedani, Yefta na Samweli

Haya ni majina ya baadhi ya waamuzi ambao Mungu aliwainua.

1 Samuel 12:12

'Hapana! Badala yake, mfalme awepo atawale juu yetu

Sentensi hii inaonesha namna ambavyo taifa la Israeli lilimpinga Samweli alipowaambia kuwa wamwamini Mungu kwa sababu Mungu aliwaokoa zamani.

ambaye mmemchagua, ambaye mlimuomba

Sentensi hizi zina maana moja na zinasisitiza kuwa huyu ndiye mfalme ambaye watu wanamtaka.

1 Samuel 12:14

mnamuhofu ... mtumikieni ... mtiini.... msimuasi

Maneno haya yanayofanana yametumika ili kusisitiza umuhimu wa jambo hili.

dipo mkono wa BWANA utakuwa juu yenu, kama ulivyokuwa juu ya babu zenu.

"Bwana atawaadhibu ninyi kama walivyowaadhibu babu zenu"

1 Samuel 12:16

Mbele ya macho yenu

"macho" inawakilisha watu wa taifa la Israeli.

Je, leo si mavuno ya ngano?

Samweli anajua kuwa ni wakati wa mavuno. "Ni wakati wa mavuno na mvua hainyeshi katika wakati huu"

Akatuma radi na mvua

Samweli anamuomba Bwana awaadhibu Israeli kwa kutaka mfalme kwa mumuomba atume mvua ya radi wakati wa mavuno ambayo itaharibu mavuno.

1 Samuel 12:19

Ili tusife

Adhabu ya dhambi ni kifo. Taifa la Israeli liliona Bwana akiharibu mataifa yaliyowanyanyasa. Walikuwa na wasiwasi kuwa wataharibiwa kama mataifa mengine.

Msiogope

Watu walifanya maovu na waliogopa kuwa Mungu atawaharibu. "Msiogope kuwa Mungu atakasirika na kuwaharibu kwa sababu ya dhambi hii"

msigeuke na kufuata mambo matupu

"msikimbilie kuabudu miungu ya uongo"

1 Samuel 12:22

Kwa ajili ya jina lake kuu

"Hivyo watu wataendelea kumuheshimu na kumtii Bwana"

Kwangu mimi, iwe mbali nami kumtenda BWANA dhambi kwa kuacha kuwaombea ninyi.

Watu walishikwa na hofu kwa sababu ya radi na mvua ambavyo Bwana alivituma Samweli alipoomba. Watu wengine walihisi kuwa Samweli atatumia maombi yake kuwaangamiza.

1 Samuel 13

1 Samuel 13:1

Taarifa ya jumla:

Samweli anawakumbusha watu kumfuata Bwana.

Sauli alikwa na umri wa miaka thelathini ... juu ya Israeli

Maneno katika mistari hii yamenukuliwa toka katika vitabu vya zamani hivyo kwa matoleo ya kisasa kunaweza kuwa na tafsiri ya tofauti.

Askari waliobaki aliwarudisha nyumbani

"Aliwarudisha askari waliobaki nyumbani"

Aliwachagua watu elfu tatu

"Aliwachagua watu 3,000"

Elfu mbili walikuwa pamoja naye huko Mikmashi

"2,000 walikuwa pamoja naye huko Mikmashi"

Gibea ya Benyamini

Gibea ni jina la mji.

1 Samuel 13:3

ngome ya Wafilisti

"ngome ya jeshi la Wafilisti" au "kambi ya jeshi la Wafilisti"

Geba

Hili ni jina la mji ambapo ngome ya Wafilisti ilikuwepo huko.

Israeli yote imesikia kwamba Sauli ameipiga

Hii yaweza kuwa na maana ya 1)Sauli alichukua jukumu la vitendo vya Yonathani au 2)Sauli alichukua pongezi kwa vitendo vya Yonathani.

Uvundo

Taifa la Israeli linafananishwa na uvundo.

Ndipo askari wakaitwa kwa pamoja kuungana na Sauli huko Gilgali.

"Sauli akawaita askari kwa pamoja kuungana naye huko Gilgali"

1 Samuel 13:5

elfu tatu ... elfu sita

"3,000 ... 6,000"

majeshi mengi kama mchanga ufukoni mwa bahari

Kundi la askari walikuwa wengi na ilikuwa ngumu kuwahesabu.

Mikimashi

Hili ni jina la mahali.

Beth aveni.

Hili ni jina la mahali.

1 Samuel 13:6

Taarifa ya jumla:

Wafilisti walikusanyika ili kupigana dhidi ya Israeli.

Watu

Taifa la Israeli.

watu walikata tamaa

"watu waliogopa sana"

nchi ya Gadi na Gileadi

Haya ni majina ya miji.

Walimfuata wakitetemeka

Watu walikuwa wanogopa sana.

1 Samuel 13:8

muda uliopangwa na Samweli.

"kutokana na muda ambao Samweli alimwambia kuwa atakuja"

watu wakatawanyika mbali na Sauli

"Watu wakaanza kumuacha Sauli"

Kisha akatoa sadaka ya kuteketezwa

Ukoo wa Haruni tuu ndio ulioruhusiwa kutoa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana.

1 Samuel 13:11

Umefanya nini?

Samweli alikuwa haulizi swali ila alikuwa akimkemea Sauli. Sauli akaanza kujitetea japokuwa alikosea.

Mikmashi

Hili ni jina la mahali.

1 Samuel 13:13

Taarifa ya jumla:

Sauli anamwambia Samweli kwa nini amefanya kitendo hicho kama kuhani na kutoa sadaka.

Hukuheshimu amri ya BWANA

Sauli alipaswa amsubiri Sauli afike na atoe sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana na sio kufanya hivyo yeye.

Aliutengeneza utawala wako

"Aliuweka utawala wako" au "aliuchagua utawala wako"

utawala wako hautaendelea

"Utawala wako utakoma muda si mrefu"

mtu anayekubaliwa na moyo wake

"Mtu atakayefuata amri zake"

1 Samuel 13:15

Samweli akasimama na kwenda

"Samweli akaondoka na kwenda mpaka"

mpaka Gilgali

Gilgali ni jina la mji.

Gibea ya Benyamini

Gibea ni jina la mji.

Watu mia sita

"600"

Geba ya Benyamimni

Geba ni mji.

Wafilisti wakapiga kambi huko Mikmashi

Mikmashi ni jina la mahali.

1 Samuel 13:17

Wateka nyara

Wateka nyara ni askari jeshi wanovamia vijiji vya adui zao kwa ajili ya chakula na mahitaji mengine.

Ofra, hadi nchi ya Shuali ... Bethholoni ...bonde la Seboimu

Haya ni majina ya mahali.

1 Samuel 13:19

Taarifa ya jumla:

Msimuliajia nasimulia kusuhu wafua vyuma wa Israeli.

Hakuna hata mhunzi aliyeonekana

"Hakuna mtu atakayempata mhunzi"

Mhuzni

Mhuzi ni mtu anayetengeneza vifaa vya chuma na silaha.

kunoa jembe lake

Jembe ni kifaa cha chuma ambacho hutumika kulimia ardhini kwa ajili ya kupanda mazao.

sululu ... shoka ... mundu

Hivi ni vifaa vya kwenye bustani

Sululu

Ni kifaa chenye ncha kali kinachotumika kupasulia udongo mgumu.

mundu

Ni kifaa cha ncha kali kinachotumika kukatia majani na nafaka.

Theluthi mbili ya shekeli

Shekeli imegawanywa katika sehemu tatu na mbili ya tau imetolewa.

kunyoosha michokoo

Kuondoa mchokoo na kumfanya ng'ombe anyooke ili aweze kutumika.

1 Samuel 13:22

Taarifa ya jumla

Simulizi inaendelea:

hakukuwa na mapanga au mikuki

Hii inaelezea ni kwa nini jeshi la Sauli lilikuwa linaogopa. Hawakuwa na silaha kwa ajili ya mapigano.

1 Samuel 14

1 Samuel 14:1

Taarifa ya jumla:

Yonathani anaanza uvamizi wake wa pili katika jeshi la Wafilisti.

mbeba silaha wake aliye mdogo,

Kijana mdogo aliyekuwa na jukumu la kubeba silaha za bwana wake kwa ajili ya vita.

gome ya Wafilisti

Hii ni sehemu ambayo jeshi la Wafilisti iliweka kambi.

1 Samuel 14:2

Gibea

Hili ni jina la kilima kaskazini mwa Yerusalemu.

chini ya mti wa mkomamanga

Ni mti ambao matunda yake yana ganda gumu, la duara jekundu na lenye mbegu nyingi kwa ajili ya kula.

ulio katika Migroni

Migroni ni eneo lililopo Kaskazini mwa Yerusalemu.

watu mia sita walikuwa pamoja naye

"watu 600 walikuwa pamoja naye"

mwana wa Ahitubu (nduguye Ikabodi)

"Ahitubu" n"a Ikabodi" ni majina ya wanaume.

Finehasi mwana wa Eli

Finehasi alikwa mmoja wa makuhani.

1 Samuel 14:4

Jabali moja liliitwa Bosesi

Jabali ni mwamba wenye mteremko mkali. Jabali hili lilijulikana sana na lilipewa jina la "Bosesi"

Jabali lingine liliitwa Sene

Hili lilikuwa jina la jabali lingine.

Mikmashi

"Mikmashi" ulikuwa mji kaskazini mwaYerusalemu.

Geba

"Geba" ulikuwa mji kaskazini mwaYerusalemu.

1 Samuel 14:6

kijana mbeba silaha wake

Kijana mdogo aliyekuwa na jukumu la kubeba silaha za bwana wake kwa ajili ya vita.

wasiotahiriwa

Hili ni neno lililotumika kuwaelezea watu ambao hawakuwa Wayahudi.

atatenda kwa niaba yetu

"atatusaidia"

hakuna kitu kiwezacho kumzuia Bwana asiokoe

"Bwana anaweza kuokoa"

kwa wengi au kwa watu wachache

"Kwa idadi yoyote ya watu"

kila kitu kilicho ndani ya moyo wako

"kila kitu unachotamani kufanya"

1 Samuel 14:8

hatutavuka kwenda kwao

"hatutakwenda katika upande mwingine wa bonde ambapo Wafilisti wapo"

amewaweka mkononi mwetu

"atatuwezesha kuwashinda"

Hii ndiyo itakuwa ishara yetu

"Hii itathibitisha kuwa Bwana atakuwa pamoja nasi"

1 Samuel 14:11

wakajifunua mbele ya ngome ya Wafilisti

"wakaruhusu askari wa Wafilisti wawaone"

mgome

"Kambi ya jeshi"

wanakuja kutokea kwenye mashimo walimojificha

Wafilisti wanaelezea kuwa Waebrania walijificha kwenye mashimo chini kama wanyama.

tutawaonesha jambo

"tutawafundisha jambo"

amewaweka katika mkono wa Israeli

"Atawawezesha Waisraeli kuwashinda"

1 Samuel 14:13

Yonathani alipanda juu kwa mikono na miguu yake

"Hivyo Yonathani akapanda juu kwa kutumia mikono na miguu yake kwa sababu kulikuwa na

Wafilisti waliuwawa mbele ya Yonathani

"Yonathani aliwaua Wafilisti"

mbeba silaha wake akiwaua baadhi nyuma yake

"Mbeba silaha wa Yonathani alimfuata na kuwaua askari wa Wafilisti"

1 Samuel 14:15

Kukawa na hofu

"kulikuwa na woga sana"

Wateka nyara

Wafilisti waliokuwa wakiteka nyara miji ya Israeli.

Nchi ikatetemeka

"Mungu alisababisha nchi ikatetemeka"

1 Samuel 14:16

Gibea

Hili ni jina la mji.

likitawanyika ... wakienda kule na huku

Maneno haya yanamaana sawa yakisisitiza kuwa askari walikuwa wakikimbia kila mahali.

1 Samuel 14:18

Lete hapa Sanduku la Mungu

Matoleo mapya yameandika "naivera" badala ya "sanduku la Mungu"

ghasia

"kelele nyingi na kuchanganyikiwa"

Acha kazi unayofanya

"Acha kufanya jambo unalofanya" Sauli hakutaka Ahiya aendelee kulitumia sanduku la Mungu kuulizia uelekeo"

1 Samuel 14:20

watu aliokuwa nao

Jeshi la Israeli ambalo lilibaki pamoja na Sauli.

Upanga wa kila Mfilisti ulikuwa juu ya Mfilisti mwenzake

"Wafilisti walipigana wao kwa wao kwa upanga"

1 Samuel 14:22

Waisraeli wote waliokuwa wamejificha katika milima

Askari hawa walijificha kwa sababu waliwaogopa Wafilisti.

Beth aveni

Hili ni jina la sehemu katika Israeli.

1 Samuel 14:24

Hivyo hakuna hata mmoja kati ya watu wote aliyeonja chakula

Ilieleweka kwa watu kuwa chini ya kiapo cha Sauli hakuna chakula kilichoruhusiwa.

Watu wakaingia msituni

Askari wa Wafilisti walikimbilia msituni na askari wa Israeli wakawafuata.

Asali ilitiririka

Hii inasisitiza kuwa "kulikuwa na asali nyingi kila mahali"

hakuna aliyeweka mkono wake kinywani

"hakuna aliyekula chochote"

watu waliogopa kiapo

Watu hawakukiogopa kiapo ila waliogopa adhabu iliyoambatana na kuvunja kiapo.

1 Samuel 14:27

Taarifa ya jumla:

Yonathani anagundua juu ya kiapo cha baba yake.

amewaagiza watu kwa kiapo

"aliwaamuru watu kwa kutii kiapo"

akanyoosha mkono wake hadi kinywani mwake

"Alikula asali"

macho yake yakaangaziwa

Sentensi hii inamaanisha kuwa alipata nguvu. "alirejeshewa nguvu zake"

1 Samuel 14:29

nchi

Hii inawakilisha taifa la Israeli.

Macho yangu yalitiwa nuru

Sentensi hii inamaanisha kuwa alipata nguvu. "alirejeshewa nguvu zake"

Je, siyo vizuri sana kama watu ... walizopata?

Yonathani anatumia swali hili kueleza kuwa watu walitakiwa waruhusiwe kula. "Ushindi wetu ungekuwa mzuri sana ikiwa watu wangekuwa huru kula nyara walizochukua toka kwa adui zao"

Nyara

Hivi ni vitu ambavyo watu huchukua wakiwa vitani toka kwa adui zao.

Kwa sababu sasa mauaji hayakuwa makubwa

Kwa sababu askari hawakuweza kula wakati wa vita walikuwa dhaifu. Kwa sababu hii hawakuweza kuwaua Wafilisti wengi.

1 Samuel 14:31

Taarifa ya jumla:

Maneno ya Yonathani yakawafanya watu wamtende Mungu dhambi katika njaa yao kuu.

Mikmashi

Hili ni jina la mji.

Aiyaloni

"Aiyaloni" ni sehemu huko Zebuloni Israeli.

Watu

Hawa ni Waisraeli.

walikula nyama zao pamoja na damu.

Walikuwa na njaa sana hivyo walikula mpaka damu. Hapa walikiuka sharia aliyopewa Munsa kwa ajili ya taifa la Israeli.

1 Samuel 14:33

kula pamoja na damu

Hii ilikuwa ukiukwaji wa sharia ambayo Musa alipewa kwa ajili ya taifa la Israeli.

Mmetenda isivyo haki

Sauli analishitaki jeshi lake lote kwa kutenda bila uaminifu japokuwa sio wote waliofanya hivyo.

Sasa, viringisheni jiwe kubwa kwangu

Jiwe lingewashikilia wanyama na kusababisha damu ikauke haraka kwenye miili yao.

wawachinje hapa, na kuwala

Hii ingemuwezesha Sauli kuona kuwa damu ilikauka toka kwa wanyama.

1 Samuel 14:35

Taarifa ya jumla:

Sauli anawaambia watu wawawekee wanyama jiwe kubwa ili kuwaua na kuwala.

Sauli akamjengea Bwana madhabahu

Haipo wazi kama Sauli alijenga madhabahu hii kwa jiwe kubwa ambalo watu walimletea.

1 Samuel 14:36

Taarifa ya jumla:

Sauli anataka kuendelea kupigana na Wafilisti.

tusimwache hata mtu mmoja akiwa hai

"Tumuue kila mtu"

Fanya unaloona linakupendeza

Sauli aliungwa mkono na jeshi lake katika kuendeleza mapigano.

Hebu na tumkaribie Mungu mahali hapa

"kumkaribia Mungu" ni kitendo cha kutaka ushauri kwake. " hebu tumuulize Mungu la kufanya"

utawaweka katika mkono wa Israeli

"utatusaidia kuwashinda"

Lakini Mungu hakumjibu siku hiyo

Hii inadhihirisha kuwa Mungu hakuwa tayari kumsaidia Sauli.

1 Samuel 14:38

mjue na kuona jinsi dhambi hii ilivyotokea leo

"mjue nani aliyefanya dhambi"

Watu

Hawa ni Waisraeli.

hata kama angekuwa mwanangu Yonathani, atapaswa kufa

Sauli alisema hivi kwa sababu hakuamini kuwa mwanaye Yonadhani alikuwa na makosa.

akini hakuna hata mtu mmoja miongoni mwa watu aliye mjibu neno.

Watu walikuwa kimya kwa sababu wengi wao walijua kuwa Yonathani alivunja kiapo cha Sauli.

1 Samuel 14:40

Basi akawaambia Waisraeli wote

"Akawaambia askari wa Israeli waliokuwepo hapo"

Tuoneshe Thumimu ... wakatwaliwa ... piga kura

Wakati huo Waisraeli walitumia wawe maalumu yaliyoitwa Urimu na Thumimu katika kupokea maelekezo toka kwa Mungu.

1 Samuel 14:43

Taarifa ya jumla:

Kura ilionesha kuwa Yonathani alitenda dhambi.

Niambie umefanya nini

"Niambie ni kwa namna gani umetenda dhambi" au "niambie ni kosa gani umefanya"

Nitakufa

Yaweza kuwa na maana ya 1) "nipo tayari kufa" au 2) "Je nina sitahili kufa kwa sababu ya nilichokifanya"

Mungu afanye hivyo na kuzidi hata kwangu, kama Yonathani hautakufa

Sauli alifanya tena kiapo kibaya. "Mungu na aniue kama sitakuua wewe Yonathani"

1 Samuel 14:45

Taarifa ya jumla:

Jeshi linamtetea na kumlinda Yonathani toka kwa Sauli.

Je, inampasa Sauli afe, ni nani aliyetekeleza ushindi huu mkubwa kwa ajili ya Israeli? Mbali na hayo

"Yonathani amekamilisha ushindi huu mkubwa. Hakika hatakufa"

Kama Bwana aishivyo

Watu wanaonesha uhakika wao kuwa hawataruhusu lolote limpate Yonathani.

hata unywele mmoja wa kichwa chake hautaanguka chini

Hii inaonesha kuwa Watu wa Israeli watamlinda Yonathani. "tutamlinda na mabaya yote"

1 Samuel 14:47

Taarifa ya jumla:

Kwa muda mfupi Sauli aliwapiga maadui wa Israeli.

Israeli

Israeli inawakilisha watu wa Israeli.

Moabu

Hii inawakilisha watu wa Moabu.

Edomu

Hii inawakilisha watu wa Moabu.

Popote alipogeukia

"popote alipotuma jeshi lake"

kutoka kwenye mikono

"kutoka kwenye utawala"

1 Samuel 14:49

Taarifa ya jumla:

Hii inaonesha taarifa ya familia ya Sauli.

Ishvi ... Malkishua

Haya ni majina ya wanaume.

Merabu ... Mikali

Haya ni majina ya wanawake.

Ahinoamu ... Ahimaasi

Haya ni majina ya wanawake.

Abneri ... Neri ... Kishi ... Kishi

Haya ni majina ya wanaume.

1 Samuel 14:52

Siku zote za Sauli

"maisha yote ya Sauli"

alimuunganisha kwake

"alimlazimisha kujiunga na jeshi lake"

1 Samuel 15

1 Samuel 15:1

Maneno ya Bwana

"ujumbe wa Bwana"

ukaangamize kabisa vitu vyote walivyo navyo ... ua wote mwanamme na mwanamke, mtoto na mtoto mchanga, ng'ombe na kondoo, ngamia na punda

Sentensi hizi zina maana moja. Sentensi ya pili inaelezea kwa undani vitu ambavyo vinapaswa kuharibiwa.

Usiwaache

Hii inasisitiza kuharibu kila kitu.

1 Samuel 15:4

Watu

"jeshi"

kuwahesabu

"kuwahesabu"

mji wa Talemu

Mji ulioko kusini mwa Yuda.

watu mia mbili elfu waendao kwa miguu, na watu elfu kumi kutoka Yuda

watu 200,000 waendao kwa miguu, na watu 10,000 kutoka Yuda

1 Samuel 15:6

Wakeni

Kundi la wafugaji ambalo walikuwa marafiki wa taifa la Israeli.

Havila ... Shuri

Haya ni majina ya mahali.

1 Samuel 15:8

Taarifa ya jumla:

Sauli anapuuzia maeneo ambayo Bwana aliagiza yaangamizwe.

akamchukua Agagi

"akamkamata Agagi"

ncha ya upanga

"ncha ya upanga" inawakilisha jeshi la taifa la Israeli.

Sauli ... wakamwacha Agagi

Sauli hakumtii Mungu kwa kumuacha Agagi aishi.

pamoja na kondoo wazuri

Sauli hakumtii Mungu kwa kuchukua wanyama wazuri.

Hawakuangamiza

"waliviweka kwa ajili yao wenyewe"

1 Samuel 15:10

Neno la Bwana likamjia

"Bwana akasema maneno yake"

Neno la Bwana

"ujumbe wa Bwana"

Inanihuzunisha

"Nina huzuni"

aligeuka nyuma asinifuate

"Aliacha kunifuata"

hakutekeleza maagizo yangu

"hakutii yale niliyomuamuru ayafanye"

Samweli alikasirika

Samweli alikasirika kwa sababu ya kutotii kwa Sauli.

1 Samuel 15:12

Samweli aliambiwa

"mtu alimwambia Samweli"

amejijengea ukumbusho kwa ajili yake

Sauli alikuwa na kiburi

chini hadi Gilgali

Gilgali ilikuwa chini zaidi ya Karimeli.

nimetekeleza amri ya Bwana

Haipo wazi ikiwa Sauli anaelewa kuwa hakutii amri ya Mungu ya kuwaangamiza kabisa Waamaleki.

1 Samuel 15:14

Taarifa ya jumla:

Samweli anauliza kwa nini Sauli hakuwaangamiza kabisa Waameleki.

masikioni mwangu ... ninayosikia

Maneno haya yana maana sawa. "masikioni mwangu" ina maana ya "kusikia"

kilio cha kondoo ... milio ya ng'ombe

Hii ni milio ambayo wanyama hutoa. Lugha yako yaweza kuwa na maneno tofauti.

Wao wamewaleta ... watu waliwaacha

Watu hawa wanaozungumziwa hapa ni jeshi la Sauli.

Sadaka kwa Bwana Mungu wako

Sauli anajitetea kuwa wanyama kwa ajili ya dhabihu walikuwa sababu ya kutotii amri ya Bwana ya kutoangamiza kila kitu.

Bwana Mungu wako

Sauli hapa hamuelezei Mungu wa Samweli kama Mungu wake mwenyewe.

1 Samuel 15:17

machoni pako mwenyewe

"kwa mawazo yako mwenyewe"

je, hukufanywa mkuu wa kabila za Israeli?

Samweli anatumia swali hili kumueleza Sauli ni vitu vingapi Mungu amempa. "Mungu amekufanya kuwa mtawala wa kabila za Israeli"

Kwa nini basi haukuitii ... ukafanya uovu machoni pa Bwana?

Samweli anauliza swali hili kwa kumkemea Sauli kwa kutomtii Mungu.

Sauti ya Bwana

"Vitu ambavyo Bwana ameamuru"

bali badala yake ulishikilia nyara

Samweli anamshitaki Sauli moja kwa moja kwa kutokutii.

Nyara

"Nyara" ni vitu unavyovichukua toka kwa adui.

Uovu machoni pa Bwana

"ambayo Bwana anayaona kuwa ni uovu"

1 Samuel 15:20

Kweli kabisa niliitii sauti ya Bwana.

Sentensi hii haipo wazi kama Sauli alifikiri kuwa hili ni kweli au alikuwa akijitetea kwa sababu ya dhambi yake.

Sauti ya Bwana

"Vitu ambavyo Bwana ameamuru"

Lakini watu walichukua

Hapa anahamisha lawama kwa watu.

vitu vilivyokusudiwa kuangamizwa

Wanyama ambao Bwana aliamuru waharibiwe"

Gilgali

Hili ni jina la mahali.

Agagi

Hili ni jina la mfalme wa Waameleki.

1 Samuel 15:22

Je, BWANA hufurahia sadaka za kuteketezwa na dhabihu kama ilivyo kuitii sauti yake?

Samweli alitumia swali hili kusisitiza kuwa kutii ni jambo la muhimu sana kuliko dhabihu.

Sauti ya Bwana

"Vitu ambavyo Bwana ameamuru"

Utii ni bora kuliko dhabihu

Mungu alitaka Sauli amtii kabisa kwa kuwaangamiza Waamaleki. Hakuna kilichokuwepo kwenye nchi ambacho kilifaa kwa dhabihu.

bora kuliko mafuta ya beberu

"bora kuliko dhabihu ya mafuta ua beberu kama sadaka ya kuteketezwa"

uasi ni sawa na dhambi ya uchawi

"uasi ni kama dhambi ya kufanya uchawi"

ukaidi ni sawa na uovu na udhalimu

"Kuwa mkaidi ni sawa na dhambi ya kuabudu sanamu"

umelikataa neno la Bwana

"umekataa kufanya jambo ambalo Bwana ameamuru"

amekukataa usiwe mfalme

"ameamua kuwa hautakuwa tena mfalme"

1 Samuel 15:24

nimevunja amri ya BWANA

"Sikutii aliloliamuru Bwana"

kwa sababu niliwaogopa watu

"Kwa sababu niliwaogopa askari"

kuitii sauti yao

"kufanya kile walichokiomba"

urudi nami

Sauli na Samweli walikuwa waliongea faragha mbali na watu wengine.

1 Samuel 15:26

kwa sababu umekataa neno la BWANA

Samweli anaonesha wazi kuwa Sauli ameelewa kuwa hakumtii Bwana wakati ambapo waliwaacha wanyama wazuri na hakumuua Agagi.

Umekataa neno la Bwana

"Umekataa kufanya aliloliamuru Mwana"

Sauli akashika pindo la kanzu yake

Sauli alifanya hivi ili kumzuia Samweli asiondoke.

pindo la kanzu yake

"mwisho wa kanzu yake"

1 Samuel 15:28

Bwana ameuchana ufalme wa Israeli

"Kama ulivyochana kanzu yangu vivyo hivyo Bwana ameuchana ufalme wa Israeli"

amempa jirani yako, aliye bora kuliko wewe.

Mungu ameshaamua ni nani atakuwa mfalme baada ya Sauli.

Uwezo wa Israeli

Hii inamuelezea Mungu ambaye huwapa nguvu Waisraeli.

hatasema uongo wala kubadili nia yake

Hii inasisitiza kuwa Mungu hasemi uongo.

nia yake

"alichoamua kukifanya"

si mwanadamu, kwamba abadili nia yake

"Yeye ni Mungu na atafanya alichosema kuwa atakifanya"

1 Samuel 15:30

Lakini tafadhali nipe heshima wakati huu mbele ya wakuu

Sauli alikuwa anatamani sana kuheshimiwa na watu badala ya kumwabudu Mungu.

mbele ya wakuu wa watu wangu na mbele ya Israeli

"mbele ya watu wa Israeli na viongozi wanaowaongoza"

Urudi tena pamoja nami

"Urudi pamoja nami"

Hivyo Samweli akamrudia tena Sauli

Hii inaonesha kuwa Samweli alibadili mawazo yake na akarudi pamoja na Sauli walipokuwepo watu.

1 Samuel 15:32

Agagi akafika kwake akiwa amefungwa minyororo

"walimpeleka Agagi akiwa amefungwa minyororo"

Hakika uchungu wa kifo umepita

"Kwa hakika sipo tena katika hatari au kufa"

Jinsi upanga wako ulivyofanya wanawake wapoteze watoto, vivyo hivyo mama yako naye hatakuwa na mtoto miongoni mwa wanawake

Maneno haya yana maana moja "Kwa kuwa umewaua watu, wewe pia utauawa"

ulivyofanya wanawake wapoteze watoto, vivyo hivyo mama yako naye hatakuwa na mtoto

"umewaua watoto wa wanawake wengine, hivyo nitamuua mtoto wa mama yako"

Kisha Samweli akamkata Agagi vipande vipande

Samweli aliimaliza kazi ambayo Bwana alimuamuru Samweli alifanye.

1 Samuel 15:34

Rama ... Gibea

Haya ni majina ya mahali.

akapanda kwenda nyumbani kwake Gibea

Gibea ilikuwa juu kuliko Gilgali ambapo Sauli na Samweli walikuwa wakizungumza.

Samweli hakumuona tena Sauli hadi siku ya kifo chake

Hii inaonesha kuwa Samweli alikufa mbele ya Sauli lakini hakumuona Sauli tena kipindi akiwa hai.

1 Samuel 16

1 Samuel 16:1

Utamlilia Sauli kwa muda gani, ikiwa nimemkataa asiwe mfalme juu ya Israeli?

"Acha kumlilia Sauli niliyemkataa asiwe mfalme juu ya Israeli"

Ijaze pembe yako mafuta

Pembe ilitumika mara nyingine kama chupa. Chupa ya mafuta ilitumika kwa ajili ya kumpaka mafuta mfalme, kama Samweli alivyofanya kwa Daudi.

1 Samuel 16:2

Nitakwendaje?

Samweli anatumia swali kusisitiza kuwa anaogopa kwenda Bethlehemu.

pamoja nawe na usema

"pamoja nawe mpaka Bethlehemu na uzungumze na watu wa huko"

na useme, 'Nimekuja kutoa dhabihu kwa BWANA

"na uwaambie watu wa huko kuwa umekwenda kutoa dhabihu kwa Bwana"

1 Samuel 16:4

Wazee wa mji walikuwa wakitetemeka walipokuja kuonana

Wazee walikuwa wakitetemeka kwa sababu waliogopa kuwa Samweli amekwenda kuwakemea.

Kwa amani

"ndio, nimekuja kwa amani"

Jitoeni wenyewe

"Kujitoa" inamaana ya kuwa watu wajitoe wenyewe tayari kwa ajili ya kusudi la Mungu kwa kujitakasa kutokana na sheria ya Musa.

1 Samuel 16:6

Walipofika

"Hawa ni Yese na watoto wake"

akamwangalia Eliabu

Samweli alimuangalia Eliabu.

Eliabu

Hili ni jina la moja wa wana wakubwa wa Yese.

amesimama mbele yake

Mbele ya Bwana.

Bwana haangalii kama mtu aangaliavyo.

"Kuangalia" ina maana ya kutathimini jambo.

Kwa kuwa Bwana haangalii ... Bwana anaangalia

"Kwa kuwa mimi Bwana siangalii ... Mimi Bwana naangalia"

Moyo

"Moyo" inawakilisha sehemu ya ndani ya mtu.

1 Samuel 16:8

Abinadabu ... Shama

Haya ni majina ya wana wa Yese.

akamwambia apite mbele ya Samweli

"Akamwambia aende kwa Samweli"

Kisha Yese akmwambia Shama apite

"Kisha Yese akamwambia Shama aende kwa Samweli"

1 Samuel 16:11

Yupo mdogo kabisa amesalia

"Bado yupo mtoto wangu mdogo"

hatutakaa chini

"Hatutakaa chini ili tule"

Naye ... muonekano

Hapa msimuliaji anatusimulia kuhusu mtu mwingine katika simulizi.

kijana huyu alikuwa mwekundu

Hii inamaanisha kuwa Daudi alikuwa na mwonekano wenye afya.

1 Samuel 16:13

pembe yenye mafuta

Pembe ilitumika mara nyingine kama chupa. Chupa ya mafuta ilitumika kwa ajili ya kumpaka mafuta mfalme, kama Samweli alivyofanya kwa Daudi.

Samweli akanyanyuka na kwenda

Hii inaonesha kuwa alinyanyuka baada ya kukaa na kula.

Roho wa Bwana akamwijia Daudi

Roho wa Bwana alimchochea Daudi. Roho wa Bwana alimuwezzesha Daudi kutimiza yote ambayo Bwana alimtaka ayafanye.

1 Samuel 16:14

Basi

Hapa msimuliaji anaanza kutuambia sehemu mpya ya simulizi.

roho ya ubaya kutoka kwa Bwana

"roho ya ubaya" ni "roho inayosababisha matatizo"

Haya bwana wetu hebu sasa amuru

Watumishi wanamchukulia Sauli kama bwana wao.

amuru watumishi wako walio mbele yako wamtafute

"tuamuru sisi watumishi wako tunaokutumikia tumtafute"

yuko juu yako

"anakusumbua wewe"

1 Samuel 16:17

mwenye nguvu, mtu jasiri

Yaweza kuwa na maana ya 1) "shujaa" au 2) "mtu mwenye hekima"

mwenye busara aongeapo

"anayeongea kwa busara"

Bwana yuko pamoja naye

Hii inamaanisha kuwa Bwana alimsaidia na kumbariki Daudi.

1 Samuel 16:20

Daudi akafika kwa Sauli

"Daudi akaenda kwa Sauli.

kuanza kazi yake

"na akaanza kumtumikia"

akawa mbeba silaha wake

Daudi akawa mbeba silaha wa Sauli.

1 Samuel 16:22

Mruhusu Daudi awe mbele yangu

"Kusimama mbele yangu" inamaanisha kuwa aendelee kumtumikia Sauli"

amepata kibali machoni pangu

"Nimependezwa naye"

Roho ya ubaya kutoka kwa Bwana.

"roho ya ubaya" ni "roho inayosababisha matatizo"

kiwapo juu ya Sauli

Ikamsumbua Sauli"

Sauli angeburudishwa na kupona

"Muziki ungemfurahisha Sauli na kumfanya ajisikie vizuri"

1 Samuel 17

1 Samuel 17:2

bonde la Ela

Hili ni jina la bonde.

1 Samuel 17:4

mikono sita na shubiri moja

Mkono mmoja ni sawa na sentimeta 46. Shubiri ni sawa na urefu wa sentimeta 23.

alivaa dirii ya chuma

"alijilinda mwenyewe kwa kuvaa dirii ya chuma"

Shekeli elfu tano

Shekeli ni kama ujazo wa gramu 11.

1 Samuel 17:6

mkuki wa shaba

Huu ni mkuki mdogo ambao upo kwa aliji ya kurushwa.

mpini wa mkuki wake

"mshikio wa mkuki wake"

kamba ya sindano ya mfumaji

"kamba inayozunguka"

Kichwa cha mkuki wake

"Mwanzoni wa mkuki wake"

shekeli mia sita

Yapata kilogramu 7"

1 Samuel 17:8

Kwa nini mmekuja na mmejipanga kwa ajili ya vita?

"kwa nini mmekuja kupigana dhidi yetu?" Goliati alitumia swali hili ili kuwadhihaki Waisraeli.

Mimi si Mfilisti, na ninyi si watumishi wa Sauli?

Goliati alitumia swali hili ili kuwadhihaki Waisraeli. "Mimi ni Mfilisti mkuu na ninyi ni watumishi wa Sauli"

1 Samuel 17:10

Leo ninayapa changamoto majeshi ya Israeli

"Ninalipa changamoto jeshi wa Israeli"

Israeli wote

Hawa ni askari wa Israeli waliokuwepo huko.

walikata tamaa na kuogopa sana

Maneno haya yanamaana moja ya kuonesha walikuwa na hofu kuu.

1 Samuel 17:12

alikuwa na watoto wanane

Hapa anazungumziwa Yese.

Yese alikuwa mzee ... mzee mwenye umri mkubwa

Maneno haya yanaonesha msisitizo mkubwa.

aliyemfuata Abinadabu, na watatu aliitwa Shama

"Abinadabu alikuwa mtoto wa pili na Shama alikuwa wa tatu.

1 Samuel 17:14

wakubwa watatu

"Wana wakubwa watatu wa Yese"

Kwa siku arobaini

"kwa siku 40"

akajitokeza kwa ajili ya vita

"akajitokeza kuwa yupo tayari kwa ajili ya vita"

1 Samuel 17:17

Efa

Efa ni kipimo sawa na lita 22.

jemedari kikosi chao cha elfu

Jeshi liligawanyika katika makundi ya watu elfu na kila kundi kilikuwa na jemedari.

Ukawaangalie wako na hali gani

"kaangalie na uone kaka zako wanaendeleaje"

1 Samuel 17:19

Watu wote wa Israeli

"askari wote wa Israeli"

bonde la Ela

Hili ni jina la bonde.

1 Samuel 17:22

jina lake Goliathi

"Ambaye jina lake aliitwa Goliati"

akajitokeza kutoka majeshi ya Wafilisti

"akatokeza mbele toka kwa jeshi la Wafilisti"

1 Samuel 17:25

Umemuona mtu huyu aliyejitokeza?

"Muangalie mtu huyu aliyejitokeza"

Mfalme

"mfalme wetu"

Binti yake

Huyu ni binti wa mfalme.

atampa ... nyumba ya baba yake

Huyu ni mtu atakayemuua Goliati.

ataifanya familia ya baba yake isilipe kodi katika Israeli.

"hataruhusu familia yake ilipe kodi"

1 Samuel 17:26

kuiondolea Israeli fedheha

"na akaifanya Israeli isifedheheke tena"

Ni nani Mfilisti huyu asiyetahiriwa ayatukanaye majeshi ya Mungu aliye hai?

Daudi alisema maneno haya kuonesha hasira yake kwa Wafilisti wanaolidharau jeshi la Mungu.

Mfilisti huyu asiyetahiriwa

Maneno haya yanaonesha kuwa Goliati hakuwa mtu wa Mungu aliye hai.

1 Samuel 17:28

Hasira ya Eliabu ikawaka moto dhidi ya Daudi

Hapa hasira inafananishwa na moto uwakao.

Kwa nini umekuja hapa?

Eliabu anatumia swali hili kuonesha kuwa alikuwa na hasira na Daudi.

Wale kondoo wachache umewaacha na nani huko nyikani?

Eliabu alitumia swali hili kwa kumdhihaki Daudi kwa kuonesha kuwa kazi yake haikuwa ya muhimu na kumuhukumu kwa kutokuangalia kondoo wa baba yake.

kiburi chako, na utundu wa moyo wako

Maneno haya yanaonesha msisitizo.

"Nimefanya nini sasa? Mimi si numeliuliza swali tu?

"Sijafanya jambo lolote baya, nilikuwa nauliza swali tuu"

Akamgeukia na kumuacha

Hapa Daudi aligeuka na kumuacha Eliabu.

1 Samuel 17:31

Maneno aliyosema Daudi yaliposikika

"Askari waliposikia aliyoyasema Daudi"

Pasiwepo moyo wa mtu atakayezimia

"asiwepo mtu atakayepoteza ujasiri"

Mtumishi wako atakwenda

"Mimi mtumishi wako nitakwenda"

1 Samuel 17:34

Mtumishi wako alikuwa akichunga kondoo za baba yake

Daudi anajizungumzia mwenyewe kama "mtumishi wako" kuonesha heshima kwa Sauli.

alikuwa akichunga kondoo za baba yake

"alikuwa akitunza kondoo wa baba yake"

dubu

Dubu ni mnyama mkubwa mwenye miguu minne lakini anaweza kusimama na miguu miwili kama mtu.

Nilimfukuza na kumshambulia

Hapa anazungumziwa simba au dubu.

na kumpokonya kutoka kinywani mwake

Hapa anazungumziwa mwana kondoo.

aliponirukia

"alinivamia"

nilimshika ndevu zake

"ndevu" zinamuelezea simba au nywele zilizopo katika uso wa dubu.

1 Samuel 17:36

Sentensi unganishi

Daudi anaendelea kuzungumza na mfalme Sauli.

Mfilisti asiyetahiriwa

Maneno haya yanaonesha kuwa Goliati hakuwa mtu wa Mungu aliye hai.

atakuwa kama mmoja wao

Daudi ataweza kumuua Mfilisti kama alivyoweza kumuua simba na dubu.

1 Samuel 17:37

kutoka makucha ya simba na makucha ya dubu

Simba na dubu hutumia kucha zao kuvamia hivyo "kucha" inawakilisha kuvamia.

mkono wa Mfilisti

"nguvu za Mfilisti huyu"

chepeo ya shaba

Vazi la kivita lililofunikwa kwa mabamba madogo.

1 Samuel 17:39

upanga wake juu ya vazi lake

"upanga wa Sauli juu ya vazi lake"

fimbo mkononi mwake

Hapa anamuelezea Daudi.

Kombeo lake lilikuwa mkononi mwake

Kombeo ni silaha iliyotumika kwa ajili ya kurusha mawe.

1 Samuel 17:41

mbeba ngao yake akiwa mbele yake.

"na mbeba ngao yake alikuwa mbele yake"

akamdharau

"akamchukia"

mwekundu

"mwenye afya"

Je, mimi ni mbwa, hata ukanijia na fimbo?

Mbwa anawakilisha mnyama mdogo ambaye mtu anaweza kumuua kwa urahisi. "Umenidharau kwa kunujia kwa fimbo kama vile nimekuwa mbwa"

1 Samuel 17:44

nyama yako nitawatupia ndege wa angani na wanyama wa mwituni

Goliati anazungumzia kumuua Daudi na kuacha mwili wake chini kwa ajili ya kuliwa na wanyama kama vile kuutoa mwili wa Daudi ili uliwe na wanyama.

Ndege wa angani

"ndege"

wanyama wa mwituni

"wanyama wa porini"

Kwa jina la Bwana

"kwa nguvu ya Bwana" au "kwa mamlaka ya Bwana"

uliyemdharau

"uliyemdhihaki"

1 Samuel 17:46

Sentensi unganishi:

Daudi anaendelea kuaongea na Goliati.

Nitawapa mizoga ... ndege ... na wanyama wa mwituni

Daudi anaongea katika kuwaongoza Waisraeli kuwaua Wafilisti na kuacha maiti zao katika ardhi ili wanyama wale. "Tutawaua Wafilisti na ndege wa angani na wanyama wa mwituni watawala"

dunia yote ijue

"watu wote wa duniani wajue"

Bwana hatui ushindi kwa upanga wala mkuki

Panga na mkuki ni silaha za vita. "Ushindi anaoutoa Bwana hautegemei upanga wala mkuki"

Vita ni ya Bwana

"Bwana huwa anashinda vita wakati wote"

atawaweka katika mkono wetu

"atatusaidia kuwashinda"

1 Samuel 17:50

Daudi alimshinda ... Alimpiga ... kumuua ... Mkononi mwa Daudi hakukuwa na upanga

Mstari wa 50 unaonesha ushindi wa pekee wa Daudi juu ya Goliati. Inaonesha namna ambavyo Daudi alimuua Goliati.

Ndipo Daudi akakimbia akasimama juu ya Mfilisti

Daudi alifanya hivi baada ya Goliati kuanguka chini.

Akachukua upanga wake

"akachukua upanga wa Mfilisti"

1 Samuel 17:52

Na maiti za Wafilisti walilala katika njia iendayo Shaaraimu

"Na wakawaua Wafilisti na maiti za Wafilisti katika njia iendayo Shaaraimu"

wakateka nyara kambi yao

"Waisraeli waliteka nyara kambi za Wafilisti"

akaliweka vazi la vita katika hema lake

"akaweka vazi la vita la Goliati katika hema yake"

1 Samuel 17:55

Sauli alipomuona Daudi

Mazungumzo katika 17:55-56 yalitokea kabla Daudi hajamuua Goliati.

akienda kukabiliana na yule Mfilisti

"akienda kupigana na Mfilisti"

kijana huyu ni mtoto wa nani

"baba yake na huyu kijana ni nani"

Kama uishivyo

Hii ni namna ya kuapa na kuonesha kuwa anayotaka kuyasema ni kweli.

mvulana huyu ni kijana wa nani

"baba yake na kijana huyu ni nani"

1 Samuel 17:57

mkononi mwake

Hapa anazungumziwa Daudi

wewe ni mtoto wa nani?

"Baba yako ni nani"

Mimi ni mtoto wa mtumishi wako Yese Mbethlehemu

"Baba yangu ni mtumishi wako Yese Mbethlehemu"

Mtumishi wako Yese

Daudi anatumia neno hili "mtumishi wako" kuonesha kuwa baba yake alikuwa mwaminifu kwa mfalme Sauli.

1 Samuel 18

1 Samuel 18:1

roho ya Yonathani ilishikana na roho ya Daudi

Urafiki wa karibu sana unasemwa kama unavyounganisha roho za watu wawili. Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "Yonathani alipenda sana Daudi' au 'Yonathani alijitolea kwa Daudi"

Yonathani akampenda kama roho yake mwenyewe

Hapa "kupendwa" inaonyesha upendo kati ya marafiki, si upendo wa kimapenzi. Neno "nafsi" linawakilisha mtu au maisha ya mtu. AT "Yonathani alipenda Daudi kama alivyojipenda mwenyewe" au "Yonathani alipenda Daudi kama alipenda maisha yake mwenyewe"

1 Samuel 18:3

Yonathani akampenda kama roho yake mwenyewe

Hapa "kupendwa" inaonyesha upendo kati ya marafiki, si upendo wa kimapenzi. Neno "nafsi" linawakilisha mtu au maisha ya mtu. Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 18:1. Wakati "Yonathani alipenda Daudi kama alivyojipenda mwenyewe" au "Yonathani alipenda Daudi kama alipenda maisha yake mwenyewe"

1 Samuel 18:5

naye alifanikiwa

"naye alifanikiwa"

Jambo hili lilipendeza machoni pa watu na katika macho ya watumishi wa Sauli.

Maneno "mbele ya" na "mbele ya" yanamaanisha kitu kimoja. Maoni ya watu yanasemwa kuwa kitu ambacho wanachokiona kama kizuri au mbaya. AT "Hii ilikuwa ya kupendeza katika maoni ya watu wote na watumishi wa Sauli" au "Hii iliwafaidi watu wote na watumishi wa Sauli"

1 Samuel 18:6

kutoka miji yote ya Israeli

Hii ni kufanya kusisitiza idadi kubwa ya wanawake waliokuja. AT "kutoka miji mingi katika Israeli"

wakiwa na matowazi, wenye furaha, na wakiwa na ala za muziki

"kucheza matowazi kwa furaha na ala za muziki"

wakiwa na matowazi

"matowazi" ni ngoma ndogo ya mkono

Na Daudi ameua makumi elfu yake

Kitenzi kinaweza kutolewa kutoka kwenye mstari uliopita. AT "na Daudi ameua makumi elfu"

1 Samuel 18:8

Wamemsifia

"Wameshukuru"

Atapata kitu gani zaidi isipokuwa ufalme?

Swali hili la uongo linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Kitu pekee ambacho anahitaji ni ufalme."

1 Samuel 18:10

roho ya ubaya kutoka kwa Mungu

Hapa "roho ya ubaya" inaweza kutaja "roho inayosababisha shida" au "roho ya ubaya." Tazama jinsi ulivyotafasiri hii katika 16"14.

roho ya ubaya kutoka kwa Mungu ikamwingia Sauli

Maneno "ikamuingia" yanamaanisha roho ya madhara yalisaidia Sauli. Katika kesi hii ina maana kwamba umesababisha Sauli kuwa na wasiwasi na kutenda mambo. Tazama jinsi ulivyotafasiri maneno sawa katika 10:5.

na akachukiza

"Naye akajifanya kichaa"

Bwana alikuwa pamoja nae

"Bwana alikuwa pamoja na Daudi"

1 Samuel 18:13

Hivyo Sauli alimuondoa Daudi mbele yake

"Basi Sauli akamwondoa Daudi kuondoka mbele yake"

maelfu

Hii inaweza kuwakilishwa kwa nambari. AT "watu 1,000"

David alitoka na kuingia mbele ya watu

Hapa "watu" hutaja askari chini ya amri ya Daudi. Maneno ambayo "kutoka" na "kuingia" ni maadui ambayo inahusu kuwaongoza watu katika vita na kuwaongoza nyumbani kutoka vita. AT "Daudi aliwaongoza askari wake katika vita na kuwaongoza nyumbani kutoka vita"

1 Samuel 18:15

alimwogopa

Hapa "kumwogopa" ni maneno ambayo ina maana ya hofu. AT "alimwogopa Daudi"

watu wote wa Israeli na Yuda walimpenda Daudi

Hapa "Israeli na Yuda" wanawakilisha watu wa kabila zote. AT "watu wote wa Israeli na Yuda walimpenda Daudi"

alitoka na kuingia mbele yao

Maneno ambayo "toka" na "ingia" ni maneno ambayo yanahusu kuwaongoza watu katika vita na kuwaongoza kwenda nyumbani kutoka vitani. Tazama jinsi ulivyotafasiri hii katika 18:13. AT "aliongoza askari wake katika vita na kuwaongoza nyumbani kutoka vitani"

1 Samuel 18:17

Usije mkono wangu ukawa juu yake, ila acha mkono wa Wafilisti uwe juu yake

Kumharibu mtu kunazungumzwa kama kuwachini ya mtu huyo. Hapa, Sauli anataja kumwua Daudi. AT "Mimi sio nitakaye kumwua; Nitawawezesha Wafilisti kumwua"

Mimi ni nani, na maisha yangu yana nini, au hata maisha ya familia ya baba yangu katika Israeli......kwa mfalme?

Daudi hutumia swali hili la kuvutia ili kusisitiza kuwa hastahili kuwa mkwe wa Sauli. AT "Mimi si mtu na jamaa zangu wala familia ya baba yangu ni muhimu sana kwa Israeli ... kwa mfalme."

mkwe wa mfalme

mkwe wa mfalme - "mume wa binti ya mfalme"

1 Samuel 18:19

wakati Merabu, binti ya Sauli, angepaswa kupewa Daudi

Hii inaweza kuelezwa katika fomu harisi. AT "wakati Sauli angempati Daudi binti yake Merabu"

aliozwa kwa Adrieli

Hii inaweza kuelezwa katika fomu harisi. AT "Sauli akampa Adrieli"

1 Samuel 18:20

Mikali.... alimpenda Daudi

Hapa "kupendwa" maana yake alikuwa na hisia za kimapenzi kwa Daudi.

Akamuambia Sauli

Hapa "wao" inahusisha watu ambao walijua kuhusu hisia za Mikali, si kwa Daudi na Mikali.

hivyo mkono wa Wafilisti pengine uwe juu yake

Kumharibu mtu kunazungumzwa kama kunaweka mtu chini ya mwingine. Hapa, Sauli akimaanisha kumwua Daudi. Tazama jinsi ulivyotafasiri maneno sawa katika 18:17. AT "ili Wafilisti wasimwue"

Wewe utakuwa mkwe wangu

mkwewe - "utakuwa mume wa binti yangu"

1 Samuel 18:22

watumishi wake wote wanakupenda

"watumishi wake wote wanakubali"

Sasa basi

"Kwa sababu hizi unapaswa"

1 Samuel 18:23

Kwenu ninyi mnaona ni jambo dogo kuwa mkwe wa mfalme, mimi ni maskini, na heshima yangu ni ndogo?

mkwe, kwani mimi ni mtu maskini, na ninahesabiwa kidogo? - Daudi anauliza swali hili la kuvutia ili kusisitiza kuwa hastahili kuwa mkwe wa mfalme. AT "Ni jambo kubwa kuwa mkwe wa mfalme, na mimi ni maskini sana na si muhimu kwa hilo."

1 Samuel 18:25

'Mfalme haitaji mahari yoyote, isipokuwa govi mia moja

Kitenzi cha maneno ya pili inaweza kutolewa kutoka kwa ya kwanza. AT "Mfalme hataki zawadi yoyote; anahitaji tu kwamba unamletea govi 100"

govi

"mahali". Katika utamaduni huu, mtu huyo alihitajika kutoa zawadi kwa baba mkwe.

govi

Neno "govi" linamaanisha ngozi ya kwenye sehemu za siri ambayo inaondolewa wakati wa kutahiriwa.

ili ajilipize kisasi kwa adui wa mfalme

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "kulipiza kisasi juu ya maadui wa mfalme"

kumfanya Daudi kuangukia kwenye mikono ya Wafilisti

Hapa "kuanguka" maana yake kufa. Neno "mkono" linawakilisha Wafilisti. Hii inaweza kuelezwa katika fomu harisi. AT "Wafilisti kumuua Daudi"

1 Samuel 18:27

Wafilisti mia mbili

Hii inaweza kutafsiriwa kwa nambari. AT "200 Wafilisti"

kumkadhi mfalme kulingana na idadi yake

"Daudi na watu wake wote waliwapa mfalme"

Sauli akaona, na akajua

Hapa maneno "kuona" na "kujua" yanashiriki maana sawa na kusisitiza kwamba Sauli alijua kwa uhakika. AT "Sauli alijua"

Mikali, binti Sauli, akampenda

Hapa "kupendwa" maana yake alikuwa na hisia za kimapenzi kwa Daudi.

1 Samuel 18:30

hivyo jina lake likapata heshima kubw

Hapa "jina" ni msamiati kwa Daudi. Hii inaweza kuelezwa katika fomu harisi. AT "ili watu wamheshimu sana Daudi"

1 Samuel 19

1 Samuel 19:1

watumishi wake wote

Hapa "wake" inamhusu Sauli.

alimfurahia sana Daudi

Yonathani alifurahi sana kuwa na Daudi.

1 Samuel 19:4

Mfalme asije akafanya dhambi dhidi ya mtumishi wake

Yonathani anaongea kama Sauli ni mtu mwingine kuonyesha Sauli kwamba Yonathani anamheshimu Sauli. AT "Usitende dhambi dhidi ya mtumishi wako"

alijitoa maisha yake

Hapa "kujitoa maisha yake" ni idiom ambayo inahusu kuhatarisha maisha yake. AT "alihatarisha maisha yake"

Kwa nini utende dhambi juu damu isiyo na hatia kwa kumuua Daudi bila sababu?

Yonathani anauliza swali hili kumkemea Sauli. Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "hupaswi kutenda dhambi dhidi ya damu isiyo na hatia na kumwua Daudi bila sababu."

dhambi juu damu isiyo na hatia

Hapa "damu" ni muhimu kwa maisha ya mtu asiye na hatia. AT "kufanya dhambi ya mauaji"

1 Samuel 19:6

yeye hatauawa

Hii inaweza kuelezwa katika fomu harisi. AT "Sitamwua" au "Sitamwua" au "Nitamfanya awe hai"

alikuwa mbele yake

Daudi alikuwa mbele ya Sauli.

1 Samuel 19:8

Yule roho mchafu kutoka kwa Bwana

Hapa "roho mchafu" inaweza kutaja 'roho inayosababisha shida" au "roho mchafu." Tafsiri kama katika 16:14.

1 Samuel 19:10

kumpigilia Daudi ukutani kwa mkuki

kutupa mkuki wake uweze kupita kwa Daudi na kwenye ukuta

anaweza kumwua

"Sauli anaweza kumwua Daudi"

Mikali.... akamuambia

Mikali alimwambia Daudi

Usipoyaokoa maisha yako

Hapa "Usipoyaokoa maisha yako" ni tendo ambalo linahusu kutoroka. AT "Ikiwa hutatoroka"

utauwawa

Hii inaweza kuelezwa katika fomu harisi. AT "mtu atakuua"

1 Samuel 19:12

Taarifa ya jumla

Mikali anamsaidia Daudi kumtoroka Mfalme Sauli. Anatumia sanamu ili kuonekana kwamba Daudi aonekane kuwa amelala kitandani.

akaweka mto wa singa za mbuzi kichwani pake, na akakifunika na nguo

Inawezekana maana ni 1) kichwa cha sanamu kilikuwa kimelala mto wa nywele za mbuzi na Mikali amevaa sanamu katika nguo za Daudi au 2) Mikali alitumia nguo za Daudi kama kifuniko ili kufunika kabisa sanamu na akafanya "mto" wa nywele za mbuzi kuonekana kama nywele za Daudi zikidondoka chini ya blangeti ya nguo.

1 Samuel 19:14

Taarifa za jumla

Sauli anaonyesha tamaa yake ya kumwua Daudi

akamchukua Daudi

'"akamrudisha Daudi kwa Sauli"

yeye akamuambia

Hapa "yeye" inamhusu Mikali.

Mleteni kwangu akiwa kitandani

Sababu kwa nini watu walidhani Daudi alikuwa kitandani inaweza kuwekwa wazi. AT "Ikiwa yeye ni mgonjwa sana hawezi kuja kwangu, uniletee akiwa kitandani"

1 Samuel 19:16

singa za mbuzi

Kama tafsiriwa katika 19:12.

tazama

Neno "tazama" hapa linaonyesha kwamba wajumbe walishangaa kwa kile walichoona.

Kwa nini umenidanganya na kumwachilia adui yangu aende, na tena ametoroka?

Maana iwezekanavyo ni 1) Sauli anataka kujua kwa nini Mikali alifanya kile alichofanya au 2) Sauli anatumia swali hili kumkemea Mikali. Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Wewe haukupaswa kunidanganya na kuruhusu adui yangu aende, kwa hiyo ametoroka."

Acha niende. Kwa nini nikuuwe?

Ijapokuwa Daudi hakuweza kusema, Mikali anamwambia Sauli kwamba Daudi alimtishia kwa swali hili. Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Mimi nitakuua ikiwa hunisaidia kuktoroka."

1 Samuel 19:18

Taarifa za jumla

Daudi anamkimbia Samweli.

Sasa

Neno hili linatumika hapa kuonyesha kwamba mwandishi ameanza kuongea sehemu mpya ya hadithi.

Nae Sauli akaambiwa

Hii inaweza kuelezwa katika fomu harisi. AT "Mtu alimwambia Sauli"

Tazama

"Angalia" au "Sikiliza" au "Jihadharini na kile ninachokuambia"

akisimama kama kiongozi wao

Hapa "kichwa" inahusu nafasi ya mamlaka. AT "akifanya kama kiongozi wao"

1 Samuel 19:21

Sauli alipoambiwa hivyo

Hii inaweza kuanza katika fomu harisi "Pale mtu alipomuambia Sauli hivyo"

Rama....Seku...Nayothi

Haya ni majina ya mahari

1 Samuel 19:23

Kwa sababu hii, wanasema, "Je! Sauli pia ni mmoja wa manabii?"

Hii ikawa miongoni mwa Waisraeli. Inaonekana watu walisema hii kueleza mshangao wakati mtu bila kutarajia alifanya kitu ambacho hakuwa amefanya kabla. Maana ya swali inaweza kuelezwa waziwazi. Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 10:11. AT "Hiyo ndio sababu wakati watu wanapoona mtu akifanya jambo ambalo haliwezekani, wanasema," Je! Sauli pia ni nabii"

wanasuliza

Hapa "wao" inahusu watu kwa ujumla. Swali lilikuwa maelekezo kati ya watu.

1 Samuel 20

1 Samuel 20:1

Nimefanya nini? Uovu wangu ni upi? Dhambi yangu ni ipi kwa baba yako, inayofanya atafute kuutoa uhai wangu

Maswali haya matatu yanamaanisha jambo sawa. Daudi anawatumia ili kusisitiza kwamba hakumfanyia chochote kibaya kwa Sauli. Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "sijafanya chochote kibaya. Sijafanya uovu wowote. Sijafanya dhambi dhidi ya baba yako. Yeye hana sababu ya kuchukua maisha yangu."

kwamba anataka kuutoa uhai wangu?

Hapa "kuchukua maisha yangu" ni maana ya "kuniua."

Mbali na hayo

Hapa "mbali na hayo" ni dhana inayoelezea kwamba si kweli. AT "Hii si kweli"

hakuna chochote kikubwa au kidogo

Maneno "kubwa au ndogo" yanajumuisha kila kitu katikati. AT "hakuna chochote"

Kwa nini inamlazimu baba yangu anifiche jambo hili?

Yonathani anatumia swali hili kusisitiza kwamba Sauli angemwambia kama angepanga kumwua Daudi. Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Baba yangu hana sababu ya kuficha jambo hili kwangu" au "Ikiwa jambo hili ni kweli, baba yangu hakika nitanijulishe"

La, siyo hivyo

"Si kweli"

1 Samuel 20:3

Nimepata kibali machoni pako

Hapa macho yanawakilisha kuona, na kuona inawakilisha mawazo au hukumu. AT "Nimekupendeza wewe" au "unaniona vizuri"

atakuwa mwenye huzuni

Hii inaweza kuelezwa katika fomu harisi. AT "hii itashuhudia yeye" au "atakuwa na huzuni sana"

kuna hatua moja tu kati yangu na mauti

Hapa "hatua kati yangu na mauti" ni msemo ambao unahusu kuwa karibu sana na mauti. AT "Mimi ni karibu sana mauti"

1 Samuel 20:4

Taarifa za jumla

Daudi anapendekeza jaribu dhidi ya Mfalme Sauli kwa Yonathani

Kesho ni siku ya mwezi mpya

Siku ya kwanza ya mwezi kila mwezi watu walisherehekea na kutoa sadaka kwa Mungu.

hadi siku ya tatu jioni

"mpaka jioni ya siku ya kesho"

1 Samuel 20:6

Sentensi Unganishi

Daudi anaendelea kuelezea jaribu analopendekeza.

aliuliza kuondoka kwangu

"aliniuliza kama nitamruhusu aondoke"

anasema ... yeye ni ... ameamua

Neno "yeye" linamaanisha Sauli.

mtumishi wako atakuwa na amani

Daudi anazungumza mwenyewe kama ni mtu mwingine kuonyesha kwamba anamheshimu Yonathani. AT "Mimi, mtumishi wako, nitakuwa na amani"

1 Samuel 20:8

Sentensi Unganishi

Daudi anaendelea kuongea na Yonathani.

na mtumishi wako ... nimemleta mtumishi wako

Daudi anajiambia mwenyewe katika mtu wa tatu kama aina ya unyenyekevu. "Na mimi, mtumishi wako ... amenileta, mtumishi wako "au" pamoja nami ... amenifanya"

umemweka mtumishi katika agano la BWANA pamoja na wewe

Ni nini ambacho wanaume wawili walikubaliana juu yao wanaweza kufanywa wazi. AT 'Yahweh alisikia wakati ulifanya makubaliano mazuri na mimi kwamba wewe na mimi tutakuwa marafiki mara zote'

maana kwa nini basi unipeleke kwa baba yako?

Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "basi hapakuwa na sababu ya kunileta kwa baba yako"

La hasha!

Huu ni msemo ambao una maana kwamba haitafanyika kamwe kwako. AT "Hii haitafanyika kamwe kwako!"

siwezi kukuambia?

Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Mimi hakika nitakuambia."

1 Samuel 20:12

Tazama

"kuangalia" au "kusikiliza" au "kuwa makini kwa kile ninachokuambia"

ikiwa kuna mapenzi mema

"kama baba yangu anataka kufanya mambo mema kwa ajili yenu"

je, nisikutumie taarifa na kulidhihirisha kwako?

Yonathani anatumia swali hili kusisitiza kwamba atamwambia Daudi ikiwa Sauli anataka kumdhuru. Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "basi nitalituma kwenu na kukujulisha"

Bwana atamfanyie Yonathani na zaidi

Huu ndio idiom. Jonathan hutumia kiapo hiki kwa kusisitiza na anajishughulisha mwenyewe kama alikuwa mtu mwingine. AT "Bwana atanifanyia chochote kilichomdhuru baba yangu ananakusudia kukufanyia, na hata zaidi ya hayo"

1 Samuel 20:14

Taarifa za jumla

Yonathani anamwomba Daudi asiwauwe kabisa watoto wake wote ili mabaki yasalie.

hautanionesha uaminifu wa agano la BWANA, kwamba siwezi kufa?

Yonathani anauliza swali hili kuthibitisha kwamba Daudi atafanya jambo hili. Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Tafadhali unionyeshe uaminifu wa agano la Bwana, ili nisipate kufa"

nionesha uaminifu wa agano la Bwana

"Nionyeshe aina ya uaminifu wa agano kwamba Bwana anaonyesha"

nyumba ya Daudi

Neno "nyumba" ni metonym kwa watu wanaoishi ndani ya nyumba. AT "familia ya Daudi"

Bwana awe na uhasimu kutoka kwa mkono wa maadui wa Daudi

Mkono ni kingo kwa mtu. Maana iwezekanavyo ni 1) "Na Bwana awatumie maadui wa Daudi kumuadhabu ikiwa Daudi atavunja ahadi hii" au 2) "Na Bwana awaangamize maadui wa Daudi."

1 Samuel 20:17

alimpenda kama alivyopenda roho yake mwenyewe

Hapa "roho yake mwenyewe" anajielezea mwenyewe. AT "Yonathani alimpenda Daudi kama alivyojipenda mwenyewe"

Hautakuwapo

Hii inaweza kuelezwa katika fomu harisi. AT "Baba yangu atakukosa"

wakati shughuli ikifanyika

Hapa "shughuli ikifanyika" ni idiom ambayo inahusu wakati kila kitu kilichotokea. AT "wakati kila kitu kilichotokea"

jiwe la Ezeli

"Ezeli" ilikuwa jina la jiwe. AT "jiwe ambalo watu huita Ezeli"

1 Samuel 20:20

Sentensi Unganishi

Yonathani anaendelea kusema na Daudi.

kwa upande wake

Hapa neno "wake" linamaanisha jiwe ambalo Daudi alikuwa amejificha.

kijana wangu ... kijana mdogo

Hizi zinarejea mtu huyo huyo.

Tazama

"Sikiliza" au "Kuwa makini na kile nitakachokuambia"

ndipo uje

"ndipo wewe, Daudi, uje"

1 Samuel 20:22

Sentensi Unganishi

Yonathai anaendelea kusema na Daudi.

Tazama

Neno "tazama" hapa linaongeza mkazo kwa kifuatavyo. AT "kweli"

Bwana yupo kati yangu na wewe

Maana iwezekanavyo ni 1) "Bwana ni shahidi kati yako na mimi' au "Bwana ataangalia jinsi tunavyogusa" au 2) "Na Bwana awe shahidi kati yako na mimi" au "Je! Bwana angalia jinsi tunavyohusika kila mmoja nyingine" '^^

1 Samuel 20:24

Yonathani alisimama wima

Nakala za zamani zimekuwa na "Yonathani ameketi karibu naye" (UDB).

1 Samuel 20:26

Hayuko safi; hakika hayuko safi

Kwa mujibu wa sheria ya Musa, mtu asiye najisi kwa sherehe sio kushiriki katika sikukuu mpaka kuhani atangaza kwamba yeye ni safi. Sauli anarudia maneno haya kama anajaribu kujihakikishia.

1 Samuel 20:28

aliniomba ruhusa aende

"aliniuliza nitamruhusu aende"

kama nimepata kibali machoni pako

Hapa macho yanawakilisha kuona, na kuona inawakilisha mawazo au hukumu. kama ilivyotafsiriwa katika 20:3. AT "Nimekufurahia wewe" au "unaniona vizuri"

meza ya mfalme

Yonathani anamzungumzia Sauli kama kwamba yeye ni mtu mwingine kuonyesha kwamba anamheshimu Sauli. AT "meza yako"

1 Samuel 20:30

Hasira ya Sauli iliwaka yakuteketezwa dhidi ya Yonathani

Hapa "hasira ya kuteketezwa" ni metonymy ambayo inamaanisha kuwa hasira sana. AT "Sauli alimkasirika sana Yonathani"

Wee mwana wa mwanamke mkaidi na muasi!

Huu ndio mfano. Sauli anatumia maneno haya kama adhabu kali kwa Yonathani na wasiwasi wake kwa Daudi. AT "Wewe mwana mjinga wa kahaba" au "Wewe mjinga mjinga"

Wadhani kwamba sijui kuwa umemchagua Mwana wa Yese ......chi wa mama

Sauli anatumia swali hili kusisitiza kwamba anajua kwamba Yonathani na Daudi ni marafiki. Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Najua kwamba umemchagua mwana wa Yese ... uchi wa mama."

aibu ya uchi wa mama yako

Hapa "uchi wa mama" ni msemo ambao unamhusu mama aliyekuzaa. AT "kwa aibu ya mama yako aliyekuzaa"

siyo wewe wala ufalme wako utakaoimarika

Hii inaweza kuelezwa katika fomu harisi. AT "huwezi kuwa mfalme na hautaanzisha ufalme wako"

1 Samuel 20:32

Kwa sababu gani inampasa kuuwawa? Amefanya nini?

Jonathan anajaribu kumtia Sauli kufikiria kwa makini kuhusu kile anachofanya. Hii inaweza kutafsiriwa kama taarifa, na maneno "anapaswa kuuawa" yanaweza kutafsiriwa kwa fomu harisi. AT "Huna sababu nzuri ya kumwua. Hakufanya chochote kibaya." au "huna sababu ya kumwua. Hakufanya chochote kibaya."

siku ya pili ya mwezi

Hii "pili" ni namba ya upeo ambayo inahusu mbili. AT "siku ya pili ya tamasha mwezi"

alimhuzunikia Daudi

Hii inaweza kuelezwa katika fomu harisi. AT "alikuwa akimhuzunikia Daudi"

alikuwa amemwaibisha

Hapa "yeye" anaelezea Daudi.

1 Samuel 20:35

kijana alikuwa pamoja naye

Hapa "yeye" ina maana ya Yonathani.

alipiga mshale zaidi yake

"Yonathani alipiga mshale zaidi ya kijana"

mshale hauko mbele yako?

Yonathani hutumia swali hili kusisitiza kwamba mshale ni mbele zaidi ya huyo kijana. Matumizi ya kutafsiri pia inasisitiza hili. Swali la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Unapaswa kujua kwamba mshale ni zaidi ya wewe" au "Mshale ni mbali na wewe"

1 Samuel 20:38

akamwita yule kijana, "Upesi,

"alimwita kijana huyo, ambaye alikuwa akikimbia kutoka kwake," Upesi"

1 Samuel 20:41

kilima

Inaonekana kwamba Daudi alikuwa akificha nyuma ya rundo la ardhi au mawe (tazama UDB).

akiwa amelala kifudifudi, akainama mara tatu

Daudi akainama mbele ya Yonathani, ambaye alikuwa bado mwana wa Mfalme, anastahili heshima hiyo. Pia, hii ndiyo mara ya mwisho Daudi alikutana na Yonathani.

Bwana awe awe kati yako na mimi

Maana iwezekanavyo ni 1) "Yahweh ni shahidi kati ya yako na mimi" au "Yahweh ataangalia jinsi tunavyogusa' au 2) "Na Bwana awe shahidi kati yako na mimi" au "Je! Bwana angalia jinsi tunavyohusika kila mmoja nyingine. Tafsiri kama ilivyo katika 20:22.

1 Samuel 21

1 Samuel 21:1

Nobu

jina la mahari

Ahimeleki

jina la mtu

kutetemeka

kutetemeka kwa hofu

kwa jambo

"kufanya kazi kwa ajili yake"

Nimewaelekeza vijana kwenda sehemu fulani

"Nimewaambia vijana hao kwenda mahali pengine, nami nitakutana nao hapo baadaye" (Angalia UDB)

1 Samuel 21:3

Sasa basi

Daudi anaanza sehemu mpya ya mazungumzo.

chakula gani kinapatikana hapa?

Hapa "kwa upande" ni metonymy ambayo ina maana inapatikana. AT "Ni chakula gani ambacho unaweza kunipa?"

Nipatie mikate mitano

Hili ni ombi la heshima.

mkate wa kawaida

mkate ambao makuhani hawakutumia katika ibada

mkate mtakatifu

mkate ambao makuhani wametumia katika ibada

kama vijana hawajatembea na wanawake.

Hii inaweza kutafsiriwa kama hukumu kamili. AT "Wanaume wako wanaweza kula kama hawajalala na wanawake hivi karibuni"

1 Samuel 21:5

wanawake wamewekwa kutoka kwetu

Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu. AT "tumejiweka wenyewe kwa wanawake"

siku tatu

3 siku

nilipo ondoka

mimi nilipoanza safari

miili ya vijana iliwekwa wakfu

Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu ya kazi. AT "Wanaume waliweka vile ambavyo vimetengwa"

Je, si zaidi sana leo miili yao ikawekwa wakfu

Hii ni kauli, sio swali. Inaweza kutafsiriwa kwa fomu ya kazi. AT "Ni kweli hasa leo kwamba wataweka wakfu vile walivyo navyo"

mkate ambao uliwekwa wakfu

Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu ya kazi. AT "mkate ambao makuhani walikuwa wameweka"

kilicho ondolewa mbele za Bwana, ili waweke

Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu ya kazi. AT "ambayo makuhani waliondoa mbele ya Bwana ili waweze kuweka"

1 Samuel 21:7

Doegi.......wachungaji

Unaweza kuhitaji kusema wazi kwamba Doegi aliona kile Daudi alichofanya. AT " Doegi ... wachungaji, na aliona kile Ahimeleki alivyofanya"

Doegi

jina la mwanaume

ameshilkiliwa mbele za Bwana

Maana iwezekanavyo ni 1) "kwa kuwa Bwana amemzuia hapo," labda Doeg aliweza kumaliza kufanya kitu alichoahidi Bwana angekifanya (angalia UDB) au 2) hakuna mtu anayejua kwa nini alikuwa huko, "kwa sababu fulani"

wachungaji

watunzaji na walinzi wa kundi, hasa ng'ombe au kondoo

1 Samuel 21:8

Sasa hakuna hata mkuki wowote au upanga?

Hapa "upande" ni maana ya metonymy "inapatikana." AT "Je, una mkuki au upanga ambao unaweza kunipatia?" Tafsiri kama katika 21 3.

silaha

jina la jumla kwa mambo kama vile mapanga, visu, upinde na mishale, na mikuki

Bonde la Ela

Hii ndio jina la mahali pa Israeli

1 Samuel 21:10

huyu siye Daudi mfalme wa nchi hii

Walikuwa wakifanya kiburi wakati wakisema Daudi alikuwa mfalme wa nchi hiyo. Walitumia swali hili kuthibitisha kuwa Daudi alikuwa adui mwenye nguvu na Akishi hawapaswi kumruhusu awe kukaa huko. AT "Unajua kwamba hii ni Daudi, ambaye ni hatari kama mfalme wa nchi"

Je hawakupokezana kuimba na kucheza, 'Sauli ..... maelfu

Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Unajua kwamba wakati watu wa nchi walipokuwa wanacheza, waliimba kwa kila mmoja juu yake,' Sauli ... maelfu."

1 Samuel 21:12

Daudi akayaweka maneno hayo moyoni

Hapa "ilichukua ... moyoni" ni hali ya kufikiri kwa bidii juu ya kile kilichosemwa. AT "Daudi alifikiria kwa undani kuhusu yale waliyosema watumishi"

mokononi mwake

Hapa "mikono" ni metonym kwa mtu. "mbele yao"

1 Samuel 21:14

Kwa nini mumemleta kwangu?

Maana iwezekanavyo ni 1) Achish anadai kwamba watumishi wake wanasema kwa nini walimletea Daudi au 2) Akishi anawafukuza kwa swali la uwazi. AT "Unapaswa kujua kuwa hakumletea."

Kwa nini mmemleta kwangu? Je, mimi nina haja na wehu, kumbe mmemleta mtu huyu ili anifanyie hayo mbele yangu?

Swali hili la uhuishaji ni kukataa. AT "Kuna vichaa wa kutosha hapa ambao hupoteza muda wangu. Unapaswa kumleta mtu huyu awe kama mmoja mbele yangu."

Hivi kweli huyu ataingia nyumbani mwangu?

Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Usiruhusu mtu huyu aingie nyumbani mwangu."

1 Samuel 22

1 Samuel 22:1

pango

nafasi ya mashimo chini ya ardhi, kwa ujumla kufungua upande wa kilima, kubwa ya kutosha kwa watu kuingia

Adulamu

Hii ni jina la mji karibu na mji wa Gaza.

waliposikia hayo

aliposikia kwamba Daudi alikuwa amekwenda kujificha katika pango

Kila mmoja aliyekuwa na mahangaiko......kila mmoja ambaye hakuwa na furaha

Hiki ni kisichozidi. AT "Watu wengi ambao walikuwa na shida ... watu wengi ambao hawakuwa na furaha"

jemedari

afisa wa kijeshi anayeongoza askari

mia nne

"400"

1 Samuel 22:3

Kisha Daudi alitoka huko

"Ndipo Daudi akaondoka pango la Adula"

Mispa

Hii ni jina la mji.

nenda pamoja nawe

Daudi alitaka wazazi wake wapate kuishi na mfalme wa Moabu ili Mfalme Sauli asiweze kuwadhuru. Watafsiri wanaweza kueleza maana yake ya msingi kwa kutumia mawazo ya "kuja kukaa na wewe," "kukaa na wewe," au "kuishi hapa na wewe," kama katika UDB.

nenda katika nchi ya Yuda

"nenda kwenye nyumba yako ya Yuda"

Harethi

Hii ni jina la mji.

1 Samuel 22:6

Daudi amepatikana, akiwa pamoja na watu aliokuwa nao

Sauli alikuwa na hamu zaidi kwa Daudi, kwa hivyo mwandishi huwaambia watu wengine tofauti. Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu ya kazi. AT "mtu alikuwa amegundua ambapo Daudi na wanaume wote waliokuwa pamoja naye walikuwa wameficha"

mti wa mkwaju

Hii ni aina ya mti. AT "mti mkubwa wa kivuli"

huko Rama

Rama ni jina la mahali huko Gibea. Jina linamaanisha "mahali pa juu." Inawezekana maana ni 1) inaelezea hapa mahali panaitwa Ramah, au 2) inahusu sehemu yoyote ya juu. AT "kwenye kilima" (UDB)

1 Samuel 22:7

Je, mwana wa Yese atawapa mashamba na mashamba ya mizabibu?

Sauli anatumia swali ili kusisitiza kwamba Daudi, ambaye ni wa kabila la Yuda, hataki kufanya hivyo kwa watu wa kabila la Benyamini. AT "Mwana wa Yese hatakupa mashamba au mizabibu."

Je, mwana wa Yese atawapa

Wakati atakapotoa inaweza kufanywa wazi. AT "Wakati mwana wa Yese atakapokuwa mfalme, atatoa"

mwana wa Yese

"Daudi"

Je, atawafanya nyote kuwa majemedari.... mimi?

Sauli anatumia swali ili kusisitiza kwamba Daudi, ambaye ni wa kabila la Yuda, hataki kufanya hivyo kwa watu wa kabila la Benyamini. AT "Yeye hawezi kukufanya jemedari ... dhidi yangu."

Je, atawafanya nyote kuwa majemedari

Unaweza kuhitaji kutoa wazi wakati atawafanya kuwa maakida. AT "Atakapokuwa mfalme, je, atawafanya ninyi nyota majemedari"

majamedari

maofisa wa kijeshi ambao huongoza askari

1 Samuel 22:9

Doegi Mwedomu

jina la mtu. Tafsiri kama katika 21:7.

Nobu..... Ahimeleki

jina la mahali na jina la mwanadamu. Tafsiri kama katika 21:1.

Ahitubu

jina la mtu

Alimwomba BWANA ili apate kumsaidia, na alimpatia

Ahitubu akamwomba Bwana, ili Bwana amsaidie Daudi, na Ahitubu akampa Daudi

1 Samuel 22:11

kwa kumpatia

"kwa kutoa"

kuinuka

"waasi" au "kupambana"

1 Samuel 22:14

Nani miongoni mwa watumishi wako wote aliyemwaminifu kama Daudi.... nyumbani?

Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Hakuna hata mmoja wa watumishi wako ni mwaminifu kama Daudi ... nyumba."

mlinzi

mtu au kundi la watu wanaolinda mtu

mwenye heshima nyumbani mwako

Neno "nyumba" ni kielelezo kwa familia inayoishi ndani ya nyumba. Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu ya kazi. AT "ambaye familia yako inaheshimu"

Je, leo ni mara ya kwanza kwangu kumuomba Mungu apate kumsaidia?

Ahimeleki anajiuliza swali hili kabla Sauli hajaweza kuuliza, basi mara moja hujibu. Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Hii sio mara ya kwanza nimeomba kwa Mungu kumsaidia Daudi."

Iwe mbali nami!

msamiati huu una maana "kabisa"

Usimruhusu mfalme awe na shauri kwa mtumishi wake au kwa nyumba yote ya baba yangu. Kwa maana mtumishi wako hajui chochote

Ahimeleki anaongea mwenyewe katika mtu wa tatu kama "mtumishi." Ahimeleki pia anamwambia Sauli katika mtu wa tatu kama 'mfalme." Ahimeleki anaongea hivi kwa njia ya kumheshimu Sauli. AT "Tafadhali, Mfalme Sauli, usione mimi, mtumishi wako, au mtu yeyote katika nyumba ya baba yangu kuwa na hatia. Kwa maana sijui chochote "

shauri

kuzingatia mtu mwenye hatia

nyumba yote ya baba yangu.

Hapa "nyumba" inawakilisha "familia." AT "kwa familia ya baba yangu yote"

1 Samuel 22:16

nyumba ya baba yako

Neno "nyumba" ni kielelezo kwa familia inayoishi ndani ya nyumba. AT "familia ya baba yako" au "wazao wa baba yako"

mlinzi aliyesimama karibu naye

"askari wamesimama karibu ili kumlinda"

Geuka na uwauwe

Hapa "Geuka" ina maana ya kugeuka au ageuka mbali na mfalme. AT "Nenda na kuua" au "Uua"

mkono wake u juu ya Daudi

Neno "mkono" ni msisitizo kwa kazi iliyofanywa kwa mkono. AT "pia wanamsaidia Daudi"

hawakunyoosha mkono wao kuwaua

Neno "mkono" ni msisitizo kwa kazi iliyofanywa kwa mkono. AT"hakufanya chochote kuua" au "kukataa kuua"

1 Samuel 22:18

Geuka na uwauwe makuhani....akageuka na kuwapiga makuhani

Hapa "Geuka" ina maana ya kugeuka au kugeuka mbali na mfalme. Tafsiri kama katika 22:16. AT "Nenda na kuua makuhani ... akaenda na kushambulia" au "Uua kuhani ... aliwashambulia makuhani"

Doegi Mwedomu akageuka na kuwapiga..... akawauwa....... akawapiga...akawauwa

Maana iwezekanavyo ni 1) Doegi aliwauawa makuhani wote mwenyewe au 2) neno "Doegi" ni synecdoche kwa Doegi na wanaume ambao walikwenda pamoja naye. AT "Doegi na wanaume wake waligeuka na kushambulia ... waliuawa ... walishambulia ... Waliuawa"

watu themanini-watano

watu watano - "85 watu "au "85 makuhani"

Kwa makali ya upanga

"Kwa upanga"

aliishambulia Nobu

Hapa "kushambuliwa" inamaanisha kuuawa. AT "aliwaua watu wengi katika jiji la Nobu"

1 Samuel 22:20

Abiathari

Hili ni jina la mwanaume.

1 Samuel 23

1 Samuel 23:1

Kupura

Kutenganisha ngano au mbegu toka kwenye makapi.

1 Samuel 23:3

Je, si zaidi sana kama tutaenda Keila kupambana na majeshi ya Wafilisti?

"tutakuwa na hofu zaidi kama tukienda Keila kupigana na jeshi la Wafilisti."

1 Samuel 23:5

wakaenda ... kupigana ... Wakahamisha ... kuwapiga ... akawaokoa

Mwandishi anamuelezea sana Daudi hapa japikuwa watu wa Daudi walimsaidia kufanya mambo haya yote.

1 Samuel 23:7

Sauli aliambiwa

Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu. AT "Mtu alimwambia Sauli" au "Walisema Sauli"

aliita

"aitwaye" au "wamekusanyika"

1 Samuel 23:10

Daudi akasema

"Daudi aliuliza" au "Daudi aliomba"

mtumishi wako hakika amesikia....... kama mtumishi wako alivyosikia.....mwambie mtumishi wako

Daudi anaongea kama mtu mwingine aliyeonyesha heshima yake kwa Bwana. AT "Nimesikia hakika ... kama nilivyosikia ... niambie"

watanisalimisha mkononi mwake

Hapa "mkono" inawakilisha nguvu au udhibiti. AT "nipe juu ya Sauli"

kuharibu

"kushindwa kabisa"

1 Samuel 23:12

Daudi akasema

"Daudi aliuliza" au "Daudi aliomba"

watanisalimisha mimi na watu wangu katika mkono wa Sauli

Hapa "mkono" inawakilisha nguvu au udhibiti. AT "nipe mimi na watu wangu juu ya Sauli"

1 Samuel 23:13

mia sita

"600"

Sauli akaambiwa

"mtu alimwambia Sauli" au "walimwambia Sauli"

ametoroka

"amemkimbia"

hakumweka mkononi mwake

"hakumruhusu Sauli awe na nguvu juu ya Daudi" au "hakumruhusu Sauli amkamate Daudi"

1 Samuel 23:15

kuangamiza maisha yake

"kujaribu kumuua"

akamtia moyo amtumainie Mungu

akamuhimiza amuamini Mungu

1 Samuel 23:17

Kwa maana mkono wa baba yangu Sauli hautakupata

"kwa maana baba yangu hatakuwa na nguvu juu yako"

1 Samuel 23:19

Je, Daudi hakujificha kati yetu kwenye ... Yeshimoni?

"Daudi amejificha kati yetu kwenye ... Yeshimoni?

Yeshimoni

Hii ni maana nyingine ya "jangwa"

kumtia katika mkono wa mfalme

"kumleta Daudi kwako ili ufanyie kama uavyotaka"

1 Samuel 23:21

Mbarikiwe na BWANA

Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu. AT "Natumaini kwamba Bwana atakubariki"

mmenihurumia mimi

"umeniambia hii"

Jifunze na ujue

Maneno haya mawili yanamaanisha kitu kimoja na inaweza kutafsiriwa kama neno moja. AT "Fahamu kwa uhakika"

nani ambae amemuona

"nani aliyemuona"

Nimeambiwa

Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu ya kazi. AT "Watu wameniambia" au "Nimesikia"

miongoni mwa elfu zote za Yuda

Huu ndio ukweli. AT "hata ikiwa ninahitaji kumkamata kila mtu katika Yuda" au "kati ya jamaa zote za Yuda"

1 Samuel 23:24

Kisha wakasimama

Waliacha kile walichokuwa wakifanya. Msomaji haipaswi kuamini kwamba walikuwa ameketi au amelala.

Kisha wao

"Basi wazifu"

Zifu

Hili ni jina la mahali. Tafsiri hii kama ilivyo katika 23:13.

Yeshimoni

Hili ni jina la eneo la jangwa karibu na Bahari ya Ufu. Inaweza pia kutafsiriwa kama "Jangwa la Yudea" au "uharibifu." Tafsiri kama katika 23:19.

Daudi akaambiwa habari hiyo

Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu . AT "Mtu fulani alimwambia Daudi kwamba walikuwa wanakuja" au "Daudi alijifunza kwamba walikuwa wanakuja"

Mlima wa miamba

mlima uliofunikwa na miamba mingi au majabari

miongoni mwa maelfu wa Yuda

Huu ndio msemo. AT "hata ikiwa ninahitaji kumfunga kila mtu katika Yuda" au "kati ya jamaa zote za Yuda"

1 Samuel 23:26

njoo harakisha

"njoo haraka"

1 Samuel 23:28

kumfuatia

"kumkimbiza" au "kumfuata ili kumkamata"

Mwamba wa maficho

kumbukumbu au alama ya kutoroka kwa Daudim toka kwa Sauli.

1 Samuel 24

1 Samuel 24:1

Akaambiwa

"mtu akamwambia" au "wakamwambia"

elfu tatu

"3,000"

waliochaguliwa

watu waliochaguliwa kwa sababu ya uwezo wao mkubwa wa kivita

jangwa la Engedi

Engedi ni eneo kavu lililokuwa na maji katika Israeli ya mangharibu.

1 Samuel 24:3

mazizi ya kondoo

"boma la kondoo"

kujisaidia

"kwenda haja"

pango

hili ni shimo la asili lililopo chini ya ardhi na lenye uwazi kwenye upande wa kilima

Kisha Daudi akainuka na kumnyemelea kwa mbele kimya kimya

"Daudi alichukua hatua; alimnyemelea taratibu"

kunyemelea

kwenda taratibu

1 Samuel 24:5

moyo wa Daudi ukamchoma

"Daudi alihuzunika kwa sababu alitenda jambo baya"

Mtiwa mafuta wa Bwana

"mtu ambaye Bwana alimchagua kuwaongoza watu wake"

kunyoosha mkono wangu juu yake

"kumdhuru kwa namna yoyote"

1 Samuel 24:8

Kwa nini unawasikiliza watu ambao wanasema, "Angalia, Daudi anatafuta kukudhuru?

"Hupaswi kuwasikiliza watu wanaosema, 'angalia Daudi anatafuta kukudhuru.?"

1 Samuel 24:10

macho yako yameona

Hapa "macho yako" yanawakilisha Mfalme Sauli. AT "umeona kwa macho yako mwenyewe"

alivyokuweka mkononi mwangu

Neno "mkono" ni msisitizo ya udhibiti. AT "kukuweka ambapo ningeweza kukuua au kuruhusu kuishi"

Baba yangu

Sauli hakuwa baba halisi wa Daudi. Daudi anamwita "baba" kuonyesha kwamba anamheshimu Sauli.

hakuna uovu au uasi katika mkono wangu

Daudi anaongea kama uovu na uasi ni vitu vya kimwili ambavyo angeweza kushikilia mkononi mwake. Hapa "mkono" unawakilisha mtu anayefanya au kufanya kitu fulani. AT "Sikufanya chochote kibaya juu yenu, wala sijui juu yenu"

1 Samuel 24:12

mkono wangu hautakuwa juu yako

"kumdhuru kwa namna yoyote"

wazee

"watu walioishi zamani"

1 Samuel 24:14

Mfalme wa Israeli ametoka kumuandama nani? Unamsaka nani?

Swali hili linaweza kutafsiriwa kama sentensi "acha niwaambia mfalme wa Israeli amekuja kumuandama nani. Acha niwaambie ni nani unayemsaka."

Unasaka mzoga wa mbwa

"Unamsaka mtu ambaye hana nguvu kama mbwa aliyekufa"

Unasaka kiroboto

"Unasaka mtu asiye na umuhimu kama kiroboto"

ukaione na ukaitetee sababu yangu

Yaweza kuwa na maana ya 1) "kufanya yaliyo sawa na kutetea sababu yangu" au 2) "kuona kuwa sababu yangu ipo sawa na kupigana kwa ajili yangu"

toka kwenye mkono wako

"ili usiwe na nguvu juu yangu"

1 Samuel 24:16

Mwanangu Daudi

Sauli anazungumza na Daudi kama vile ni mtoto wake kumuonesha Daudi kuwa anampenda.

alinyanyua sauti yake akalia

"alilia kwa nguvu"

1 Samuel 24:17

umenitendea mema

Sauli anakiri kwamba Daudi alionyesha kwamba aliunga mkono Mfalme Sauli na alikuwa mwaminifu kwake kwa kutomwua.

kwa kuwa hukuniua wakati BWANA aliponiweka katika rehema yako

Sauli anakubali kwamba Daudi alichagua kuonyesha huruma na alionyesha uaminifu wake kwa Mfalme Sauli kama mafuta ya Bwana.

1 Samuel 24:19

Kwa kuwa mtu akimpata adui yake, atamwacha aende zake salama?

"Kama mtu akimpata adui yake hatamuacha aende salma"

9Kwa kuwa mtu akimpata adui yake, atamwacha aende zake salama?

Sauli alipoamini kuwa Daudi alikuwa adui yake na akatambua kuwa japokuwa Daudi atakuwa mfalme, Daudi hatachukua ufalmetoka kwa Sauli bali atasubiria muda wa Bwana wa kuchaguliwa.

ufalme wa Israeli utaimarika

"Bwana ataimarisha ufalme wa Israeli" au "Ufalme wa Israeli utaimarika"

katika mkono wako

"kwa mamlaka yako" au "kupitia kazi utakazozifanya"

1 Samuel 24:21

hutawakatilia mbali uzao wang baada yangu

"hutawaua wana wangu na familia zao." Ilikuwa ya kawaida kwa mfalme mpya ambaye hakuwa na mstari wa familia uliopita ili kuua watoto wote wa mfalme wa zamani ili kuzuia yeyote kati yao kumsababisha kiti cha enzi.

hautaliharibu jina langu katika nyumba ya baba yangu

Ni muhimu kwa kila familia katika Israeli kuwa na uzao kutoka kizazi hadi kizazi kinachoendelea jina la familia na urithi wa nchi. AT "huwezi kuharibu familia yangu na uzao" au "utaruhusu familia yangu kuishi"

Daudi na watu wawke

"Daudi na jeshi lake"

1 Samuel 25

1 Samuel 25:1

Waisraeli wote wakakusanyika pamoja na kumwomboleza

Hii inawezekana kuwa kizazi. Idadi kubwa ya watu wa Israeli walikuwa labda huko, lakini wengine hawakuweza kuhudhuria.

wakakusanyika pamoja

wakakutana pamoja

wakamzika nyumbani kwake huko Rama

Inawezekana maana ni kwamba walimzika Samweli 1) katika mji wake wa Rama au 2) katika ardhi ya familia yake huko Rama lakini si kimwili ndani ya nyumba au 3) nyumbani kwake huko Rama.

Daudi akainuka na akashuka

"Daudi na watu wake wakaondok na wakashuka"

1 Samuel 25:2

Kulikuwa na mtu mmoja huko Maoni, na mali zake zilikuwa huko Karmali. Mtu huyo alikuwa tajiri sana. Alikuwa na kondoo elfu tatu na mbuzi elfu moja. Naye alikuwa akiwakata manyoya kondoo wake huko Karmeli. 3Na mtu huyo aliitwa Nabali, na jina la mke wake aliitwa Abigaili. Mwanamke huyo alikuwa mwenye busara na mzuri kwa sura. Lakini mwanaume alikwa mkaidi na mwovu katika mambo yake. Alikuwa wa uzao wa nyumba ya Kalebu.

Baadhi ya watafsiri wanaweza kuweka mawazo haya tofauti. "Kulikuwa na mtu jina lake Nabali, mzao wa nyumba ya Kalebu, aliyekuwa tajiri sana. Aliishi Maoni lakini mali zake zilikuwa Karmali: Alikuwa na kondoo elfu tatu na mbuzi elfu moja. Mtu huyu alikuwa mkaidi na muovu. Mke wake aliitwa Abigaili. Mwanamke huyu alikuwa na busara na mzuri wa sura. Sasa alikuwa akiwakata manyoya kondoo wake.

Maoni

Hili ni jina la mji.

Karmali

Hili ni jina la mji.

Elfu tatu

"3,000"

elfu moja

"1,000"

akiwakata manyoya kondoo wake

"kuwanyoa sufu kondoo wake"

1 Samuel 25:4

akiwakata manyoya kondoo wake

"kuwanyoa sufu kondoo wake"

mkamsalimie kwa jina langu

"mumsalimie kama ambavyo mimi ningemsalimia nimkiwa pale"

Uishi katika baraka

"ninatamani kuwa uishi katika mafanikio"

Uwe na amani na nyumba yako iwe na amani, na wote ulionao

"ninatamani kuwa amani iwe kwako, kwa nyumba yako na vyote unavyomiliki"

1 Samuel 25:7

unao wakata manyoya

"wakata manyoya wako wanafanya kazi" Daudi alitaka watu wake wamwambie hivi Nabali ili afahamu kuwa kondoo wake wapo salama kwa sababu watu wa Daudi waliwasaidia kuwalinda.

hatukuwafanyia ubaya, na hawakupotelewa kitu chochote

Daudi anaonesha ni kwa namna gani yeye na watu wake waliwalinda watumishi wa Nabali na mifugo yao.

Basi vijana wangu wapate kibali machoni pako

"Basi ukapendezwe na vijana wangu"

kwa mtumishi wako

Daudi anaonesha heshima mbele ya Nabali kwa kuwaita watu wake watumishi wa Nabali.

mwanao Daudi

Daudi anazungumza kama vile ni mtoto wa Nabali ili kuonesha heshima kwa Nabali aliyekuwa mtu mzima.

1 Samuel 25:9

vijana wa Daudi

"jeshi la Daudi"

walimwambia Nabali yote haya kwa niaba ya Daudi

"wakampa Nabali ujumbe wote"

Daudi ni nani? Na ni nani mwana wa Yese?

Nabali alimfahamu Daudi ni nani lakini hakutaka kumsaaidia Daudi. "Huyu Daudi mwana wa Yese mnayemzungumzia ni nani ... simfahamu."

wanaotoroka

"wanaowageuka" au "wanaoasi dhidi ya"

mkate wangu

Hapa "mkate" umetumika kama aina yoyote ya chakula.

watu wanaotoka nisikokujua

"watu nisiofahamu wanatoka wapi" au "watu nisiowafahamu"

1 Samuel 25:12

kilichosemwa

"alichokisema Nabali"

akawaambia watu wake

"akaliambia jeshi lake"

ajifunge upanga wake." Kila mtu akajifunga upanga wake. Daudi naye pia akajifunga upanga wake.

"jiandaeni kwa ajili ya vita" Na kila mtu akajiandaa kwa ajili ya vita. Daudi naye akajiandaa.

mia nne

"400"

mia mbili

"200"

walibaki kulinda mizigo

Walibaki katika kambi yao ili kulinda wavamizi wasije kuiba mali zao.

1 Samuel 25:14

kijana mmojawapo alimwambia Abigaili, mke wa Nabali akasema

"Mmoja wa watumishi wa Nabali aligundua kitu ambacho Daudi na watu wake walipanga kufanya, hivyo akaenda kwa mke wa NAbali Abigaili"

Hatukudhurika

"hakuna mtu aliyetudhuru" au "tulikuwa salama"

na hatukupoteza chochote wakati wote tulipotembea nao

Watu wa Daudi waliwazuia wanyama wa mwituni na watu wengine wasiibe mifugo ya Nabali.

1 Samuel 25:16

Walikuwa ukuta

Watu wa Daudi walikuwa kama ukuta unaozunguka mji ambao unawalinda watu wa mji huo toka kwa adui zao.

ubaya unamvizia bwana wetu

"mtu anapanga kumfanyia mambo maovu bwana wetu"

bwana wetu

Mzungumzaji anazungumza juu ya Daudi kwa kuonesha kuwa anamuheshimu Daudi.

1 Samuel 25:18

mia mbili

"200"

mikate

Boflo ya mkate ni kama keki ya mkate.

waliokwisha andaliwa

"kitu ambacho kimekwisha pikwa" au "tayari kwa mtu kukipika"

vipimo

vipimo

bisi

"bisi iliyopikwa"

vishada vya zabibu

"zabibu nyingi"

1 Samuel 25:20

Daudi na watu wake

Daudi na jeshi lake

kwa kifuniko cha mlima

Maana iwezekanavyo ni 1) kwenye kitanda cha chini cha mto mkondo au 2) ambapo watu walikuwa wameficha.

1 Samuel 25:21

Taarifa ya jumla:

Mwandishi anatupa taarifa kabla hajaendelea na simulizi.

Basi Daudi alikuwa amesema, "Hakika ... wa kwake"

Msomaji anatakiwa aelewe kuwa Daudi alisema maneno haya kabla hajasema "Kila mtu afunge upanga wake" katika 25:12

Basi Daudi

Neno "basi" linaonesha kuwa mwandishi ameacha kuandika kuhusu Abigaili na akaanza kuandika kuhusu Daudi.

na vyote alivyonavyo hakuna kilichopotea

"Bado anacho kila kitu ambacho ni chake"

Mungu na anitendee hivyo mimi

"Mungu awapige adui wa Daudi"

wote wa kwake

"watu wote ambao wako chini yake" au "wale wa familia yake"

1 Samuel 25:23

Sentensi Unganishi

Mwandishi amekamilisha kutoa maelezo ya historia, hivyo anaendelea na hadithi.

akaweka mbele ya Daudi na akainama chini ya ardhi

Abigaili alikuwa akijinyenyekeza na kuonyesha kwamba angeitii Daudi kwa sababu alikuwa kiongozi mwenye nguvu

nisikilize

"sikia"

bwana wangu.... mtumishi wako....maneno ya mtumishi wako

"wewe ... maneno yangu." Abigaili anazungumzia mwenyewe na Daudi kama kwamba ni watu wawili tofauti kuonyesha kwamba anaheshimu Daudi.

1 Samuel 25:25

Taarifa ya jumla

Abigaili anaendelea kumshauri Daudi asilipe kisasi.

Nakusihi bwana wangu usimjali ... mimi mjakazi wako ... vijana wa bwana wangu ... bwana wangu ... bwana wangu

Abigaili anajizungumzia mwenyewe kwa Daudi kama vile ni watu wawili ili kuonesha heshima kwa Daudi.

Lakini mimi ... sikuwaona ... uliowatuma

"Lakini kama ... ningewaona ... uliowatuma, Ningewapa chakula"

kumwaga damu

kuua

kulipiza kisasi kwa mkono wako mwenyewe

"kulipiza kisasi mwenyewe badala ya kumuachia Bwana afanye"

adui zako ... wawe kama Nabali

Abigaili anazungumza kama vile Bwana amekwisha muadhibu Nabali. "Natumaini kuwa Bwana atawaadhibu adui zako ... kama atakavyomuadhibu Nabali"

1 Samuel 25:27

Taarifa ya jumla:

Abigaili anaendelea kumuomba Daudi asikasirike.

zawadi hii

Hata hivyo "zawadi" zilikuwa nyingi.

mtumishi wako ... bwana wangu ... bwana wangu ... kosa la mjakazi wako ... bwana wangu ... bwana wangu

Abigaili anajizungumzia mwenyewe kwa Daudi kama vile ni watu wawili ili kuonesha heshima kwa Daudi.

wapewe vijana

"tafadhali wape vijana"

Hakika Bwana atamfanyia bwana wangu nyumba imara.

"Bwana atahakikisha kuwa wazao wa bwana wangu watatumika kama wafalme.

anapigana vita ya Bwana

"anapigana dhidi ya adui wa Mungu:"

uovu hautaonekana ndani yako

"hakuna mtu atakayekuona ukifanhya uovu wowote" au "hautafanya uovu wowote"

1 Samuel 25:29

kukuandama

"kukimbiza" au "kuwinda"

uhai wa bwana wangu utafungwa katika furushi la walio hai na Bwana Mungu wako

"Bwana Mungu wako atayafunga maisha ya bwana wangu katika furushi la walio hai" au "Bwana Mungu wako atakuweka hai pamoja na walio hai"

Maisha ya Bwana wangu

Abigaili anajizungumzia mwenyewe kwa Daudi kama vile ni watu wawili ili kuonesha heshima kwa Daudi.

atayatupa maisha ya adui zako mbali, kama vile kutoka katika mfuko wa kombeo.

"Atawaua adui zako kwa urahisi kama mtu anayetupa kombeo umbali mrefu"

Kombeo

Ni kipande cha ngozi ya mnyama chenye kamba ndefu kwenye miisho yote ambapo mtu anaweza kuweka jiwe na kulirusha umbali mrefu.

1 Samuel 25:30

Senetensi Unganishi

Abigaili anaendelea kujadiliana na Daudi.

bwana wangu.... bwana wangu.....bwana wangu...mtumishi wako

Abigaili anazungumzia mwenyewe na Daudi kama kwamba ni watu wawili tofauti kuonyesha kwamba anaheshimu Daudi. "wewe ... wewe ... wewe ... mimi"

Hii haitakuwa mzigo mkubwa sana kwako

Abigaili anasema kwamba kama Daudi akichagua kutolipa kisasi atakuwa na dhamiri safi wakati Bwana atomfanya awe mfalme wa Israeli. Hii inaweza kuelezwa kwa fomu nzuri. AT "Utakuwa na furaha daima ulifanya kama ulivyofanya"

Bwana atakapomtendea bwana wangu mema

Hiyo ni, wakati Bwana amemfanya awe mfalme baada ya utawala wa Sauli kuisha.

1 Samuel 25:32

Taarifa ya jumla:

Daudi anakubali ushauri wa Abigaili na zawadi zake.

Bwana ... abarikiwe yeye

Hii inaweza kutafsiriwa kama 1) "Namtukuza Bwana ... yeye" au 2) "watu wote wamtukuze Bwana ... yeye"

Na hekima yako imebarikiwa, nawe umebarikiwa, kwa sababu

"Namshukuru Bwana kwa sababu amekubariki wewe kwa kukupa hekima na kwa sababu"

kumwaga damu

mauaji

kwa mkono wangu mwenyewe

"kwa matendo yangu mwenyewe"

1 Samuel 25:34

Taarifa ya jumla:

Daudi anakubali zawadi za Abigaili na anakubali kufanya kama alivyoshauriwa.

kwa hakika asinge salia hata mtoto mmoja wa kiume kwa Nabali

"Nisingemuachia Nabali hata mtoto mmoja mwamaume"

akavipokea kutoka mkononi mwake

"akakubali zawadi zote ambazo aliletewa"

nimeisikiliza sauti yako

"nimesikiliza ulichoniambia nifanye" au "nitafanya kama ulivyonishauri"

1 Samuel 25:36

kulipopambazuka

alfajiri

moyo wa Nabali ulifurahi ndani yake

Nabali alikuwa na furaha sana

1 Samuel 25:37

Taarifa ya jumla:

Bwana anamuhukumu Nabali

divai ilipokuwa imemtoka Nabali

"Nabali hakuwa amelewa tena hivyo hakuwa na furaha tena"

moyo wake ukafa ndani yake

Nabali alishindwa kusogea kwa sababu aliogopa sana afya yake haikuwa nzuri tena yamkini kwa sababu alipata mshtuko.

1 Samuel 25:39

Taarifa ya jumla:

Daudi anajitoa kumlinda Abigaili kwa kumuoa.

Bwana abarikiwe

(1) "namtukuza Bwana" au 2) "watu wote wamtukuze Bwana"

aliyenichukulia hatua ya shutuma yangu kutoka mkono wa Nabali

"aliyenitetea baada ya Nabali kunidhihaki"

aliyenichukulia hatua ya shutuma yangu

Hii yaweza kuwa na maana ya "amenionesha kuwa nililokuwa nalifanya lilikuwa sahihi kwa Kumuadhibu Nabali aliyenidhihaki"

na kumzuia mtumishi wake asifanye maovu

Daudi anazungumza hivi kuonesha heshima kwa Bwana "alinizuia nisifanye uovu"

Na amemrudishia Nabali tendo la uovu juu ya kichwa chake mwenyewe

"amemfanyia Nabdali jambo ambali Nabali alipanga kunifanyia"

juu ya kichwa chake mwenyewe

"juu yake"

akawatuma wakaongee na Abigaili, ili amchukue awe mke wake

"akawatuma watu waongee na Abigaili na kumwambia kuwa Daudi anataka kumchukua awe mke wake.

1 Samuel 25:41

aliinuka, akainamisha uso

Abigaili aliitikia kwa kuinamisha kichwa. Msomaji anatakiwa afahamu kuwa alikuwa amekwisha simama wanaume wale walipokuwa wakiongea naye.

Tazama, mjakazi wako ni mtumwa aoshaye miguu ya watumishi wa bwana wangu

Abigaili anazungumza hivi kuonesha heshima. "tazama mimi nitakutumikia, mtumishi wa bwana wangu Daudi, kwa kuosha miguu yako"

Akaharakisha na kuamka

Haraka alifanya alichopaswa kufanya kwa ajili ya kujiandaa na safari kisha akaamka.

watumishi wake watano waliofuatana naye

Abigaili alikuwa amepanda kwenye punda lakini watumishi wake walitembea

1 Samuel 25:43

Daudi pia alimchukua Ahinoamu ... Sauli alikuwa amempa Palti

Matukio haya yalitokea kabla Daudi hajamuoa Abigaili.

Palti ... Palti

Haya ni majina ya wanaume.

Mikali

Hili ni jina la mwanamke

Galimu

Huu ni mji uliopo kaskazini mwa Yerusalemu.

1 Samuel 26

1 Samuel 26:1

Je, Daudi hakujificha ... jangwa?

"Daudi amejificha ... jangwa!"

mbele ya jangwa

"ambapo unaweza kuliona jangwa"

jangwa

Maana nyingine ni nyika.

Sauli akaamka na kwenda

Sauli akachukua hatua; akaenda"

elfu tatu

"3,000"

watu waliochaguliwa

watu waliochaguliwa kwa sababu ya uwezo wao katika vita"

1 Samuel 26:3

mbele ya jangwa

"ambapo unaweza kuliona jangwa"

jangwa

Maana nyingine ni nyika.

1 Samuel 26:5

Daudi akaamka na kwenda

"Daudi alichukua hatua; akaenda"

Abneri ... Neri

Haya ni majina ya wanaume.

1 Samuel 26:6

Ahimeleki ... Abishai

Haya ni majina ya wanaume.

Seruya

Jina la mwanamke.

nitashuka ... mpaka

Inaonekana kuwa Daudi na watu wake walikuwa kilimani.

Mimi nitashuka

"nitaka kuwa mmoja ambaye nitashuka"

Mungu amemweka adui yako mkononi mwako

"Mungu amekupa kumtawala kabisa adui yako"

nimchome mkuki nimtoboe hadi chini kwa mkuki

"kumuua kwa mkuki"

Sitampiga mara mbili

"sihitaji kkumpiga mara ya mbili"

1 Samuel 26:9

awezaye kunyoosha mkono wake dhidi ya mtiwa mafuta wa BWANA na asiwe na hatia?

"Hakuna awezaye kumpiga mpakwa mafuta wa BWANA na asiwe na hatia"

Kama Bwana aishivyo

"kama kweli Bwana aishivyo"

siku ya kufa kwake itakuja

"atakufa kifo cha kawaida"

1 Samuel 26:11

ninyooshe mkono wangu dhidi ya

"kufanya chochote kumdhuru"

tuondoke

Daudi anamjumuisha Abishai.

sababu usingizi mzito kutoka kwa Bwana uliwaangukia

Bwana alisababisha walele usingizi mzito.

1 Samuel 26:13

Hujibu neno, Abneri?

"Nijibu, Abineri!"

kelele

"kuongea kwa nguvu"

1 Samuel 26:15

Wewe siye mtu jasiri?

"wewe ni mtu jasiri"

Ni nani yuko kama wewe katika Israeli?

Swali hili laweza kutafsiriwa kama sentensi likiwa na maana ya 1) Daudi anaendelea kumkemea Abineri "wewe ni mtu mkuu katika Israeli" au 2) Daudi anaendelea kumwambia Abineri "unataka watu wote wafikiri kuwa wewe ni mtu mkuu sana katika Israeli, lakini siyo."

hukumlinda ... mfalme?

Swali hili linaweza kutafsiriwa kama sentensi. Yaweza kuwa na maan ya 1) Daudi anataka Abneri ajibu au 2) "ulipaswa kumlinda ... mfalme."

1 Samuel 26:17

Mwanangu

Sauli hakuwa baba yake na Daudi. Sauli anazungumza kama vile alikuwa baba yake na Daudi kuonesha kuwa anataka Daudi amuamini na amtii kama vile Daudi anavyomuamini na kumtii baba yake.

Kwa nini bwana wangu anamwandama mtumishi wake?

"bwana wangu hana sababu yoyote ya kumwandama mtumishi wake"

Nimefanya nini?

Yaweza kuwa na maana ya 1) Daudi anataka Sauli amjibu swali hili au 2) "unajua kabisa sijafanya lolote kukudhuru."

Mkononi mwangu kuna uovu gani?

Yaweza kuwa na maana ya 1) "unajua kuwa sijafanya lolote bata kwako" au 2) "unaona kuwa sijapanga kukufanyia lolote baya"

1 Samuel 26:19

nakusihi, bwana wangu mfalme asikilize maneno ya mtumishi wake ... mfalme wa Israeli

"wewe mfalme wangu, sikiliza maneno yangu ... wewe"

amekuchochea dhidi yangu

"kusababisha wewe uwe na hasira juu yangu"

aikubali sadaka

"nitampa sadaka ili asisababishe tena uwe na hasira juu yangu"

Walaaniwe mbele za Bwana

"Bwana aamue kuwaadhibu"

maana leo wamenifukuza, nisishikamane na urithi wa Bwana; wameniambia, 'Nenda ukaabudu miungu mingine.'

"kwa maana leo wamenifukuza. Kwa sababu wanataka nisishikamane na urithi wa Bwana. Wameniambia 'nenda ukaabudu miungu mingine'"

usiiachilie damu yangu ianguke ardhini

"usiniue"

kiroboto mmoja

Daudi alitumia neno "kiroboto" kuonesha kuwa mtu au yeye mwenyewe hawezi kufanya madhara makubwa. "mimi sitakudhuru tena kama kiroboto mmoja awezavyo"

nisishikamane na urithi wa Bwana

"kwamba nisiamini tena kuwa Bwana atanipa mimi alichoniahidi"

kama vile mtu awindavyo kware milimani

Sauli alimkimbiza Daudi kama vile anawinda mnyama wa maana wa mwituni.

1 Samuel 26:21

Rudi

Yaweza kuwa na maana ya 1) "rudi unitumikie katika mahali pangu" au "rudi nyumbani kwako"

Mwanangu

Sauli hakuwa baba yake na Daudi. Sauli anazungumza kama vile alikuwa baba yake na Daudi kuonesha kuwa anataka Daudi amuamini na amtii kama vile Daudi anavyomuamini na kumtii baba yake.

maisha yangu yalikuwa yenye thamani machoni pak

"umeonesha kuwa unaniheshimu kabisa"

nimetenda upumbavu

"nimekuwa mpumbavu"

1 Samuel 26:22

Bwana likuweka mkononi mwangu

"Bwana alinipa nafasi ya kukuvamia leo"

amlipe

"heshima" au "tuzo"

mtiwa mafuta wake

"aliyechaguliwa kuwa mfalme"

1 Samuel 26:24

maisha yako yalikuwa ya thamani machoni mwangu

"nimekuonesha kuwa ninakuheshimu"

hivyo maisha yangu yathaminiwe sana machoni pa Bwana

"na Bwana ayathamini maisha yangu kama vile nilivyoyathamini maisha yako"

Na ubarikiwe

"Na Bwana akubariki"

mwanangu

Sauli hakuwa baba yake na Daudi. Sauli anazungumza kama vile alikuwa baba yake na Daudi kuonesha kuwa anataka Daudi amuamini na amtii kama vile Daudi anavyomuamini na kumtii baba yake.

1 Samuel 27

1 Samuel 27:1

Daudi alisema moyoni mwake

"Daudi alifikiri mwenyewe"

nitaponyoka kutoka mkono wake

"nitamtoroka yeye"

1 Samuel 27:2

Daudi akaondoka na kuvuka

"Daudi alichukua hatua; akavuka"

kuvuka

"akavuka mpaka kati ya Israeli na Philistia"

Watu mia sita

"600"

Sauli akaambiwa

"mtu alimwambia Sauli" au "Sauli alisikia"

1 Samuel 27:5

Kama nimepata kibali machoni pako

"kama nimekupendeza" au "kama utanitendea wema"

wanipatie mahali

"tafadhali nipatie mahali"

mojawapo ya miji ya nchi

"mojawapo ya miji nje ya jiji"

kwa nini mtumishi wako akae pamoja na wewe katika mji wa kifalme?

"Mimi sio wa muhimu sana mpaka nikae pamoja na wewe katika mji wa kifalme"

Mtumishi wako

Daudi anazungumza kwa kuonesha heshima kwa Akishi.

1 Samuel 27:8

wakiteka nyara

Mara nyingi walivamia na kuchukua mali.

Wagirizi

Kundi la watu waliokuwa wakiishi kati ya Filistia na Misri.

uelekeo wa kwenda Shuri

"njiani ambapo watu wengi walisafiri kuelekea Shuri"

Shuri

Ni mkoa uliokuwepo kaskazini mwa mpaka wa Misri.

Akishi

Mfalme wa Gathi.

1 Samuel 27:10

Akishi

Mfalme wa Gathi.

Wayerameeli,

Ukoo toka kabila la Yuda.

Wakeni

Kundi la watu lililoishi katika nchi ya Midiani.

1 Samuel 27:11

Gathi

Moja ya miji mikuu mitano ya Wafilisti.

Akishi

Mfalme wa Gathi.

1 Samuel 28

1 Samuel 28:1

jeshi

Kundi kubwa la majeshi.

Daudi akamwambia Akishi, "Sasa ... kufanya." Akishi akamwambia Daudi, "Basi ... mlinzi."

Neno "basi" linaonesha kuwa mzungumzaji amekubaliana na mtu mwingine kwa aliyoyasema. "Daudi alimwambia Akishi kuwa, 'kwa sababu umesema hivyo, ... fanya.' Akishi akawambia Daudi, 'kwa sababu umefanya hivyi, ... mlinzi.'"

utajua kile ambacho mtumishi wako anaweza kufanya

Daudi alitaka Akishi afikiri kuwa Daudi atawaua Wafilisti wengi, lakini "mtumishi wako anaweza kufanya" inamaana kuwa Daudi alipanga kuwaua Wafilisti.

Mtumishi wako

Daudi anazungumza kwa kuonesha heshima kwa Akishi.

Nitakufanya

Hapa anazungumziwa Daudi.

mlinzi

"mtu anayemlinda mtu mwingine"

1 Samuel 28:3

Sasa Samweli ... na pepo

Mwandishi anaonesha mwanzo wa simulizi ili kumuandaa msomaji kwa ajili ya matukio yanayofuata.

amewafukuza kutoka nchini

Kuondolewa rasmi toka kwenye nchi au mji au kuzuiwa kuingia.

wale walioongea na wafu au pepo

Maneno haya "wale walioongea na wafu" yatafsiri kwa neno moja kwa lugha asili na maneno "wale walioongea na pepo" pia tafsiri neno moja kwa lugha ya asili. Kama lugha yako ina neno moja lenye maana ya wale wanaoongea na pepo au wale wanaoongea na wafu unaweza kutumia maneno haya hapa.

Wafilisti walijikusanya

Baada ya Daudi na Akishi kuzungumza.

akawakusanya Israeli wote pamoja,

"akakusanya jeshi lake lote katika Israeli pamoja"

Shunemu ... Gilboa

Haya ni majina ya mahali.

1 Samuel 28:5

aliogopa na moyo wake ukatetemeka sana

Maneno haya yana maana sawa na yanasisitiza hofu aliyokuwa nayo.

Urimu

Kuhani mkuu alibeba kura takatifu inayoitwa Urimu na Thumimu katika ngao yake.

kuongea na wafu

Maneno haya yatafsiri kwa neno moja la lugha ya asili. Kama lugha yako ina nono moja kwa mtu anayezungumza na wafu unaweza kutumia neno hilo hapa.

Endori

Hili ni jina la mahali.

1 Samuel 28:8

Sauli akajigeuza ... akaondoka... yule mwanamke wakati wa usiku

Sauli alijigeuza kwa sababu njia ya kutoka Giboa kwenda Endori ilikuwa ya kupitia mahali ambapo Wafilisti waliishi. Alisafiri siku nzima na kumfikia mwanamke baada ya jua kuzama.

Kujigeuza

Kubadilisha mwonekano wake wa kawaida ili mtu yeyote asimtambue.

wale wanaoongea na wafu au mizimu

Maneno haya "wale walioongea na wafu" yatafsiri kwa neno moja kwa lugha asili na maneno "wale walioongea na mizimu" pia tafsiri neno moja kwa lugha ya asili. Kama lugha yako ina neno moja lenye maana ya wale wanaoongea na mizimu au wale wanaoongea na wafu unaweza kutumia maneno haya hapa.

Nitabirie ... na wafu

"ongea na waliokufa kwa niaba yangu"

Maisha yangu

Neno "maisha" inasimama badala ya mtu.

1 Samuel 28:13

mungu

Yaweza kuwa na maana ya 1)"Hakuna kama Mungu" au 2) "hakimu"

1 Samuel 28:16

amerarua ufalme kutoka mkononi mwako

"amemfanya mtu mwingine kuwa mfalme katika nafasi yako"

1 Samuel 28:18

BWANA atamweka Israeli pamoja na wewe katika mkono wa Wafilisti

"Bwana atawaruhusu Wafilisti wawafanyie chochote wanachotaka kuwafanyia wewe pamoja na watu wa Israeli"

mtakuwa pamoja nami

Hii ni njia nzuri ya kumwambia Sauli kuwa atakufa.

BWANA pia ataliweka jeshi la Israeli katika mkono wa Wafilisti

"Bwana atawaruhusu Wafilisti wawafanyie chochote wanachotaka kuwafanyia jeshi la Israeli"

1 Samuel 28:20

kwa kuwa siku hiyo alikuwa hajala chakula, hata kwa usiku huo wote

Sauli hakula chakula usiku kabla ya safari kutoka Gilboa mpaka Endori, wala mchana wakati wa safari wala usiku alipokwenda kumtembelea mwanamke.

Nimeyaweka maisha yangu mkononi mwangu na nimeyasikiliza

"Ninaweza kufa kwa sababu nimesikiliza"

1 Samuel 28:22

sauti ya mjakazi wako mwanamke

Mwanamke anazungumza kwa namna hii kuonesha kuwa anamuheshimu Sauli.

alikataa

"hakukubali" au "hakufanya kama walivyomuomba"

wakamlazimisha

"wakamuhimiza"

1 Samuel 28:24

ndama mnono

Ndama ambaye amekua na amelishwa kuwa tayari kwa ajili ya sikukuu maalumu.

yeye ... akaukanda

Alichanganya unga na mafuta, akachanganya ma mikono yake ili kutengeneza unga kwa ajili ya kuoka.

1 Samuel 29

1 Samuel 29:1

chemchemi

Ni mkondo mdogo wa maji unaotoa maji toka ardhini.

wakapita na mamia kwa maelfu

"akaenda pamoja na kundi la mamia kwa kundi la maelfu"

mamia ... maelfu

100 ...1,000

Daudi na watu wake wakapita wakiwa wa mwisho pamoja na Akishi

Kundi la watu mamia na ma walipita kwanza kisha Akishi na wasaidizi wake na Daudi, watu wake na askari wengine wa Wafilisti waliokuwa wakimlinda Akishi.

1 Samuel 29:3

Hawa Waebrania wanafanya nini hapa?

Yaweza kuwa na maana ya 1) "hukupaswa kuwaruhusu Waebrania hawa, adui zetu kuwa hapa pamoja na sisi." au 2) "Tuambie Waebrania hawa ni akina nani."

Huyu si Daudi ... kwa miaka hii ... hadi leo

Hii ina maana ya "Unatakiwa kufahamu kuwa huyu ni Daudi ... miaka hii. Nimeona ... siku hii.."

nami nimeona hana kosa

"Sijui lolote baya alilolifanya" au "Nimependezwa naye sana"

1 Samuel 29:4

usimruhusu aende nasi vitani

"usirihusu jeshi lake liungane na jeshi letu dhidi ya adui zetu"

Kwa jinsi gani mtu huyu angeweza kufanya amani na bwana wake? Siyo kwa gharama ya vichwa vya watu wetu?

"Njia pekee ya Daudi kufanya amani na Bwana wake ni kwa kuua askari wetu!"

1 Samuel 29:5

Je, huyu siye Daudi ambaye walimuimba kwa kupokezana na kucheza, wakisema, 'Sauli ... makumi elfu'?

Hii yaweza kutafsiriwa kama "hupaswi kumuamini Daudi - yeye ndiye wanayemuimba kwa kupokezana na kucheza, wakisema 'Sauli ... makumi elfu'!

elfu ... makumi elfu

"1,000 ... 10,000"

1 Samuel 29:6

Kama Bwana aishivyo

"Hii ni kauli ya kweli"

kutoka kwako na kuingia kwako pamoja nami katika jeshi ni kwema

"Nina furaha kwa sababu umetoka na kuingia pamoja nami na jeshi langu"

1 Samuel 29:8

bwana wangu mfalme

Daudi anazungumza na Akishi ili Akishi afikiri kuwa Daudi anamuheshimu. "wewe, bwana wangu na mfalme"

hata hivyo, wale wakuu

"hatahivyo, wakuu"

1 Samuel 29:10

bwana wako

Msomaji anatakiwa aelewe kuwa Akishi anamzungumzia Sauli.

kupata mwanga

"unaweza kuona kwa kutumia jua la asubuhi"

1 Samuel 30

1 Samuel 30:1

Ziklagi

Huu ni mji uliopo kusini mwa Yuda. Huku ndiko ambapo Daudi na watu wake waliziweka familia zao.

Wao

Waamaleki

Mkubwa na mdogo

Yaweza kuwa na maana ya 1) "watu wasio na umuhimu na wenye umuhimu" au 2) "watu wakubwa na wadogo"

1 Samuel 30:3

wake zao ... watoto wa kiume ... na watoto wa kike

Waliokuwa wanamuhusu Daudi na watu wake

umechomwa moto, na wake zao... binti zao walichukuliwa mateka

"waliwaona watu wakichoma moto na kuchukua wake zao ... mateka"

watu aliokuwa nao

Hawa walikuwa watu wa jeshi lake.

1 Samuel 30:5

Taarifa ya jumla:

Daudi anapata nguvu kwa Bwana baada ya uvamizi.

Ahinoamu Myezreeli

"Ahinoamu toka Yezreeli"

Nabali Mkarmeli

"Nabali toka Karmeli"

Ahinoamu ... Abigaili

Haya ni majina ya wanawake

dhiki

Mateso

roho za watu wote zilihuzunika

"watu wote walikuwa tayari kuasi dhidi ya Daudi" au "watu wote hawakuwa na furaha"

Daudi alijiimarisha katika BWANA, Mungu wake

Yaweza kuwa na maana ya 1) "Daudi alijiimarisha kwa sababu alijua kuwa Bwana Mungu wake atamsaidia" au 2) "Bwana Mungu wake alimpa nguvu Daudi"

1 Samuel 30:7

Taarifa ya jumla:

Daudi anaomba maelikezo toka kwa Bwana juu ya wavamizi wa watu wake.

Daudi akamwomba BWANA kwa ajili ya mwongozo

"Daudi alimuomba Bwana ili amwambie ni nini anapaswa kufanya"

nikiliandama

"kufukuza" au "kufuata"

1 Samuel 30:9

watu mia sita

"600"

kijito

mto mdogo

kuandama

"kufukuza" au "kufuata"

watu mia nne

"watu 400"

mia mbili

"watu 200"

waliokuwa wamechoka

Hawakuwa na nguvu tena ya kuendelea.

1 Samuel 30:11

Mmisri shambani

Aliachwa hapo ili afe na kundi la Waamaleki wavamizi.

vishada vya zabibu

"vishada vya zabibu zilizokauka"

1 Samuel 30:13

Daudi akamuuliza

Daudi akamuuliza swali mtumwa wa Misri.

siku tatu zilizopita

"siku tatu kabla"

mashambulizi

uvamizi katika mji na kuchukua mali.

1 Samuel 30:15

jeshi lililofanya mashabulizi

ni kundi la mashujaa wenye silaha wanaovamia watu au mahali ghafla.

hautaniua ... kunisaliti na kuniweka katika mikono ya bwana wangu

"hautaniua ... kuvunja uaminifu nilionao kwako kwa kumruhusu bwana wangu anitawale tena.

1 Samuel 30:16

nyara

mali zilizoibiwa katika uvamizi

jua lilipozama

muda baada ya jua kuzama mpaka anga linapokuwa na giza.

mia nne

"400"

1 Samuel 30:18

akawaokoa

"aliwaokoa" au "kuwa huru"

Hakuna kilichopotea

"hakuna kilichopotea kati ya vilivyochukuliwa na Waamaleki"

si kidogo wala kikubwa

Yaweza kuwa na maana ya 1) "watu wasio na umuhimu na wenye umuhimu" au 2) "watu wakubwa na wadogo"

nyara

mali zilizoibiwa na Waamaleki.

1 Samuel 30:21

mia mbili

"200"

kijito

mto mdogo

Besori

Hili ni jina la mto mdogo.

kumlaki

"kumkaribisha"

nyara

mali zilizochukuliwa toka kwa adui katika vita.

kurudisha

"kupata tena"

1 Samuel 30:23

Ni nani atawasikiliza kuhusu jambo hili?

"Hakuna atakayewasikiliza katika jambo hili"

Kwa maana mgawo ni kwa yeyote aendae

"kwa maana ni kwa ajili ya kila mtu aendaye"

yeyote aendae vitani

mashujaa waliopigana katika vita

watapata tena kilicho sawa

"atahakikisha kuwa kila mtu anapokea kiasi sawa"

yeyote aliyelinda mizigo

watu waliowasaidia mashujaa kutunza na kilinda vitu vyao

mzigo

vitu ambavyo mashujaa waliviacha nyuma walipokwenda vitani

1 Samuel 30:26

Taarifa ya jumla:

Mwandishi anaandika miji ambayo wazee wake walipokea zawadi toka kwa Daudi.

Ziklagi ... Bethueli ... Yatiri ... Aroeri ... Sifmothi ... Eshtemoa

Haya ni majina ya miji.

nyara

vitu ambavyo Daudi alivichukua toka kwa Waamaleki baada ya vita.

zawadi

hedaya

1 Samuel 30:29

Taarifa ya jumla:

Mwandishi anamalizia majina ya miji ambayo wazee wake walipewa zawadi na Daudi.

Rakali ... Horma ... Borashani ... Athaki

Haya ni majina ya miji.

Wayerameeli ... Wakeni

Haya ni majina ya makundi ya watu.

1 Samuel 31

1 Samuel 31:1

Basi Wafilisti wakapigana dhidi ya Waisraeli.

Vita hivi ni matokeo ya ugonvi kati ya Daudi na wafilisti katika sura ya 29:10.

Wafilisti wakapigana dhidi ya Waisraeli

"Wafilisti wakapigana dhidi ya watu wa Israeli"

mlima wa Gilboa

Hili ni jina la mlima.

wakamwandama Sauli na wanawe kwa karibu

"walimfukuza Sauli na watoto wake watatu"

Abinadabu, and Malkishua

Haya ni majina ya wanaume.

Vita vikamwelemea Sauli

"jeshi la Sauli likaanza kushindwa katika vita"

1 Samuel 31:4

mbeba silaha

Mbeba silaha alibeba ngao kubwa ya jemadari wake na silaha zingine.

hawa wasiotahiriwa

"watu hawa ambao hawajatahiriwa" au "watu ambao sio Waisraeli"

hakukubali

"hakukubali kufanya kile ambacho Sauli alimwambia afanye"

alichukua upanga wake mwenyewe na kuuangukia

"akajiua mwenyewe kwa upanga wake"

siku iyo hiyo

"siku hiyo moja"

1 Samuel 31:7

kukaa humo

kushi kwenye miji ambayo watu wa Israeli waliondoka

nyara za waliokufa

kuchukua silaha katika miili ya Waisraeli waliokufa.

Mlima Gilboa

Mlima unaoelekea bonde la Yezreeli kaskazini mwa Israeli toka Nazareti.

1 Samuel 31:9

pande zote katika nchi ya Wafilisti

"maeneo yote katika nchi ya Wafilisti"

kutangaza habari

"kuwaambia watu"

mahekalu yao ya sanamu

majengo ambayo waliabudu sanamu zao

Ashtorethi

huyu ni mungu wa uongo na sanamu

kutundika

"kubandika" (yaweza kuwa kwa kutumia msumari)

Bethi Shani

Hili ni jina la mji.

1 Samuel 31:11

Yabeshi

Hili ni jina la mji.

kile ambacho Wafilisti walimfanyia Sauli

"namna ambavyo Wafilisti walimdharau Sauli"

usiku wote

"usiku kucha"

Mkwaju

Huu ni aina ya mti, "mti mkubwa wenye kivuli"