Kiswahili: translationNotes Print

Updated ? hours ago # views See on WACS

Utangulizi wa 2 Timotheo

Sehemu ya 1 Utangulizi wa jumla

Muhtasari wa Kitabu cha 2 Timotheo

  1. Paulo anamsalimia Timotheo na kumshauri kuvumilia mateso anapomtumkia Mungu (1:1-2:13).
  2. Paulo anampa Timotheo maelekezo ya kibinafsi (2:14-26)
  3. Paulo anamuonya Timotheo kuhusu matukio yajayo na anamshauri jinsi ya kutekeleza kazi yake kwa Mungu (3:1-4:8)
  4. Paulo anatoa matamshi ya kibinafsi

Nani aliandika kitabu cha 2 Timotheo?

Paulo aliandika kitabu cha 2 Timotheo akiwa gerezani Roma. Hapo awali alijulikana kama Saulo. Alitokea mji wa Tarso. Kabla ya kuwa Mkristo alikuwa Mfarisayo na alikuwa akiwatesa sana Wakristo. Baada ya kuwa Mkristo, alisafiri mara nyingi katika himaya nzima ya Warumi akiwahubiria watu kumhusu Yesu.

Hii ni barua ya pili ya Paulo kwa Timotheo. Timotheo alikuwa mwanafunzi wake na rafiki wake wa karibu. Paulo aliandika barua hii akiwa gerezani Roma.Paulo alikuwa karibu kufa.

Kitabu cha 2 Timotheo kinahusu nini?

Paulo alikuwa amemwacha Timotheo katika mji wa Efeso ili awasaidie waumini huko. Paulo aliandika barua hii kushauri Timotheo kuhusu maswala kadhaa. Maswala aliyozungumzia katika barua hii yalikuwa: onyo kuhusu walimu wa uwongo na kuvumilia katika nyakati za matatizo. Barua hii inaonyesha jinsi Paulo alikuwa anamuandaa Timotheo kuwa kiongozi wa makanisa.

Kichwa cha kitabu hiki kitafsiriwe namna gani?

Watafsiri wanaweza amua kukiita kitabu hiki kutumia jina la asili "2Timotheo" ama wanaweza tumia kichwa cha kueleweka zaidi kama "Barua ya Pili ya Paulo kwa Timotheo", ama "Barua ya Pili Kwa Timotheo."(Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/*_tm/translate.html#translate-names)

Sehemu ya 2 Dhana muhimu za kidini na kitamaduni

Ni taswira gani ya mwanajeshi katika 2 Timotheo?

Paulo aliposubiri gerezani akiwa anafahamu kuwa angekufa muda si mrefu, alizungumzia mara nyingi kumhusu mwenyewe kama mwanajeshi wa Kristo. Wanajeshi huwajibika kwa amiri yao jinsi Wakristo wajibikao kwa Kristo. Kama "wanajeshi" wa Kristo, waumini wanapaswa kuheshimu amiri zake hata kama kufanya hivyo kutapelekea hao kufa.

Nini maana ya maandiko kuwa pumzi ya Mungu?

Mungu ndiye mwandishi halisi wa maandiko. Aliwaongoza waandishi binadamu. Hii ina maana kwamba kwa namna moja Mungu alisababisha uandishi wa maandiko na watu. Hii ndiyo maana maandiko yanajulikana pia kama neno la Mungu.Hii inamaanisha vitu vingi kuhusu Bibilia. Kwanza ni kwamba Bibilia haina kasoro na inaweza kuaminiwa. Pili, tunaweza kumtegemea Mungu kulinda maandiko kutokana na wale wanaotaka kuyaharibu. Tatu, neno la Mungu linafaa litafsiriwe katika lugha zote za dunia.

Sehemu ya 3: Maswala muhimu ya tafsiri

Umoja na wingi wa "wewe/nyinyi"

Neno "mimi" katika kitabu hiki linaashiria Paulo. "Wewe" inamaanisha Timotheo. Tofauti ya haya ni 4:22 (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/*_tm/translate.html#figs-exclusive and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/*_tm/translate.html#figs-you)

Paulo alimaanisha nini na maelezo "ndani ya Kristo" na "ndani ya Bwana" na kadhalika?

Paulo alitaka kuelezea wazo la kuwa na ushirika wa karibu sana kati ya muumini na Kristo. Tafadhali tazama utangulizi wa kitabu cha Warumi kwa maelezo zaidi kuhusu kauli hii.

Ni maswala gani kuu ya kimaandishi katika kitabu cha 2 Timotheo?

Katika aya zifuatazo,matoleo ya kisasa yanatofautiana na matoleo ya kale. Toleo la ULB lina masomo ya kisasa na imeweka masomo ya zamani kwenye tiniwayo(maelezo ya chini). Iwapo tafsiri ya Bibilia inapatikana eneo kwa ujumla, watafsiri wanashauriwa kuzingatia matumizi ya masomo yaliyoko katika matoleo hayo. Kama sivyo, watafsiri wanashauriwa kutumia masomo ya kisasa.

  • "Kwa sababu hii niliteuliwa kuwa mhubiri, mtume na mwalimu."(1:11) Matoleo mengine yanasoma, "Kwa sababu hii,niliteuliwa kuwa mhubiri, mtume na mwalimu wa watu wa Mataifa."
  • "Waonye mbele za Mungu" (2:14). Matoleo mengine ya zamani yanasoma, "Waonye mbele za Bwana."

(See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/*_tm/jit.html#translate-textvariants)

2 Timothy 1

2 Timotheo 01 Maelezo kwa jumla

Dhana muhimu katika sura hii

Watoto wa kiroho

Paulo alimfundisha Timotheo kuwa Mkristo na kiongozi wa kanisa. Kuna uwezekano kwamba Paulo pia alimuongoza kumwamini Kristo. Kwa maana hiyo Paulo anamwita Timotheo (Mwanangu mpendwa" (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/*_tw/kt.html#disciple and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/*_tw/kt.html#spirit))

Maswala mengine ya utata katika kutafsiri sura hii

Mateso makali

Paulo alikuwa gerezani wakati akiandika barua hii. Paulo anamhimiza Timotheo kuwa tayari kuteseka kwa sababu ya injili. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/*_tm/translate.html#figs-explicit)

| >>

2 Timothy 1:1

Paulo

"Toka kwa Paulo" au "Mimi, Paulo, naandika barua hii"

Kwa mapenzi ya Mungu

"kwa sababu ya mapenzi ya Mungu" au "kwa sababu Mungu anataka." Pauli alikuwa mtume kwa sababu Mungu alitakaPaulo awe mtume sio kwa sababu wanadamu walimchagua.

Sawasawa na

Inaweza kuwa na maana 1)"kuweka pamoja na," ikimaanisha kama Mungu alivyoahidi kuwa Yesu uhai, alimfanya Paulo kuwa mtume au 2) "kwa kusudi la,"ikimaanisha kuwaMungu alimteua Paulo kuwaambia wengine kuhusu ahadi ya Mungu ya uhai katika Yesu.

Ahadi ya uhai iliyo ndani ya Yesu Kristo

"Mungu aliahidi kuwafanya wale waliondani ya Kristo Yesu kuwa hai"

Mwana mpendwa

"mwana mpenzi" au "mwana apendwaye" au "mwana ninayempenda." Timotheo aliokolewa na Kristo kwa kupitia Paulo, na hivyo Paulo anamchukulia kama mtoto wake.

Neema, rehema, na amani toka

"Na neema, rehema na amani iwe kwako toka" au " Na upate neema, rehema, na amani toka"

Mungu Baba

"Mungu ambaye ni Baba yetu"

Na Kristo Yesu Bwana wetu

"na Kristo Yesu ambaye ni Bwana wetu"

Maelezo ya jumla.

Kwenye kitabu hiki neno "sisi" inawazungumzia Paulo na Timotheo pamoja na waamini wote.

2 Timothy 1:3

Ninayemtumikia, kama mababa zangu walivyofanya

Paulo alimwabudu Mungu yuleyule ambaye mababu zake walimwabudu. "...ambaye ninafanya majukumu yangu kama Mkristo kama mababu zangu waliokuja kabla yangu walivyofanya"

Kwa nia njema

"kwa nia safi." Hasumbuliwi na fikra za matendo maovu kwa sababu kila mara alijaribu kufanya yaliyo mema.

Ninapowakumbuka ninyi

"Ninapowakumbuka ninyi kila mara" au "ninapowakumbuka kila wakati"

Usiku na

inaweza kuwa na maana 1) "maombi yangu usiku na mchana" au 2) "Ninawakumbuka kila mara usiku na mchana" au 3) "natamani kuwaona usiku na mchana."

Natamani kukuona

"nasubiri sana kukuona"

Nakumbuka machozi yako

"naweka mambo yote yanayokutesa kwenye akili yangu"

Nijawe na furaha

"niwe na furaha sana" au "nifurahie"

Naikumbuka

"kwa sababu nimekuwa nikiikumbuka" au "nilipokuwa nikiikumbuka" au "kwa kuwa naikumbuka"

Imani yako iliyo thabiti

"imani yako ya kweli" au "imani isiyo ya unafiki." inamaanisha kutokuficha kitu au kuwa mkweli.

imani... iliyokuwa kwanza kwa bibi yako... ipo kwako pia

Bibi yake na Timotheo alikuwa mwanamke mcha Mungu, na Paulo anaifananisha imabi ya Timotheo na ya bibi yake.

Loisi ... Yunisi

Haya ni majina ya wanawake.

2 Timothy 1:6

Maelezo yanayounganisha:

Paulo anamtia moyo Timotheo kuishi kwa nguvu, upendo, nidhamu na kutokuona aibu kwa sababu ya mateso ya Paulo gerezani kwa sababu ya imani ya Paulo kwa Kristo.

Hii ndiyo sababu

"Kwa sababu hii" au "Kwa sababu ya imani yako ya kweli kwa Yesu" au "Kea sababu una imani ya kweli kwa Yesu"

Nakukumbusha

"Nakukumbusha wewe" au "Nakwambia tena wewe"

fufua karama ya Mungu iliyo ndani yako kwa kuwekewa mikono yangu

Paulo alimuwekea Timotheo mikono, kumkabidhi roho mtakatifu na uwezo wa kiroho au zawadi juu yake. Paulo anamwambia "afufue" ule uwezo wa kiroho kwenye kazi zake kwa ajili ya Kristo.

Kwa kuwa Mungu

"Sababu Mungu"

Mungu hakutupa roho ya woga lakini ya nguvu na upendo na nidhamu.

Paulo alipokea roho toka kwa Mungu. Alipoweka mikono yake juu ya Timotheo, roho yule yule alikuja juu ya Timotheo. Roho huyu hakusababisha wamuogope Mungu au watu wengine.

Roho wa ... nidhamu

Inaweza kumaanisha "Roho wa mungu anaweza kuwasaidia kujizuia wenyewe" au 2) "Roho wa Mungu anatusaidia sisi kuwarekebisha wengine wanaofanya makosa."

2 Timothy 1:8

Ushuhuda

"kushuhudia" au "kuwaambia wengine"

Ushiriki mateso kwa ajili ya injili

Paulo aliteseka kimakosa kwa ajili ya injili. Anamwambia Timotheo asiogope kuteseka kwa ajili ya ijnili.

Sawasawa na nguvu za Mungu

"Kumruhusu Mungu kukupa nguvu"

Sio kwa ajili ya kazi zetu

"Sio kwa sababu ya mambo mengi mazuri tuliyoyafanya tummeokolewa" au " Mungu hakutuokoa kwa sababu ya mambo mazuri tuliyoyafanya" au "Mungu alituokoa japokuwa tulifanya mambo mabaya"

Aliyetuokoa kwa mipango yake mwenyewe

"Mungu alipanga kutuokoa na sasa ametuokoa" au "Mungu aliamua kutuokoa ni vipi atatuokoa na sasa ametuokoa" au "aliyetuokoa... kama alivyopanga"

Tangu mwanzo

"Kabla ulimwengu haujaanza" au "kabla ya mwanzo"

wokovu wa Mungu umefunuliwa kwa kuja kwa mwokozi wetu Yesu Kristo

"Mungu ameonyesha namna ambavyo anaweza kutuokoa kwa kutupa mkombozi wetu Masihi Yesu kufunuliwa"

Aliyeondoa mauti

"Aliyeondoa nguvu ya kifo juu yetu"

kuleta uzima usiokwisha kwenye mwanga katika injili

"Kufundisha ni maisha gani yasiyokuwa na mwisho kwa kuhubiri injili"

Niliteuliwa kuwa muhubiri

"Mungu alinichagua kuhubiri ujumbe"

Mtumwa wake

"mtumwa kwa ajili yake" au "mtumwa kwa sababu nashuhudia habari za Bwana"

kwa Kristo Yesu

"kupitia mahusiano Yetu na Kristo Yesu"

kwa wito mtakatifu

"Tumetengwa kuwa watu wake kwa wito mtakatifu" au "kuwa watu wake watakatifu"

Alifanya haya

"alituokoa na kutuita sisi"

Kwa kuja mkombozi wety Kristo Yesu

"kwa kumtuma mkombozi wetu Yesu Kristo."

2 Timothy 1:12

Kwa sababu hii

"Kwa sababu mimi ni nabii"

Nateseka pia

Paulo anaelezea namna alivyo mfungwa.

Nina hakika

"Nina shawishika"

Siku ile

Inaweza kuwa na maana ya 1) Siku ambayo Bwana atakuja tena au 2) siku ambayo Mungu atawahukumu watu.

Utunze mfano wa ujumbe wa uaminifu uliousikia toka kwangu

"Endelea kufundisha mawazo ya kweli niliyokufundisha" au "tumia maneno yangu ma mafundisho yangu kama mfano kwa utakachofundisha"

Hilo jambo zuri

Hii inaelezea kazi ya kutangaza injili kwa usahihi.

Yatunze

Timotheo anatakiwa kuwa makini na watu wanaopinga kazi yake, wanajaribu kumkataza na kupinga nachokisema.

Kupitia roho mtakatifu

"Fanya yote na yale ambayo roho mtakatifu amekwambia uyafanye"

2 Timothy 1:15

Wameniacha

Walimuacha kwa kuwa alikuwa amekamatwa na kutupwa gerezani.

Hawakuionea aibu minyororo yangu

Onesiphorus hakumuonea aibu Paulo kwa sababu alikuwa gerezani ila alienda kumtembela mara kwa mara. "minyororo" inaelezea mtu aliyeko gerezani.

Mungu amjalie kupata neema... siku ile

Paulo anatamani Onesiphorus apokee neema na sio adhabu au 1)Siku Bwana akija tena au 2) Siku ambayo Mungu atawahukumu watu.

Figelo na Hemogene... Onesiforo

Haya ni majina ya watu.

kwenye nyumba

"kwa familia"

kupata rehema kutoka kwake

Paulo anazungumza kuhusu rehema kuwa ni jambo la muhimu la kutafta.

Siku ile

Hii inaelezea siku ambayo Mungu atawahukumu watu.

2 Timothy 2

2 Timotheo 02 Maelezo kwa Ujumla

Muundo na mpangilio

Matoleo mengine yanaweka maneno kulia kwa ukurasa kuliko maandishi mengine. ULB hufanya hivi na aya za 11-13 kuliko aya zingine. Huenda Paulo ananukuu shairi ama wimbo katika mistari hii.

Dhana muhimu katika sura hii

"Tutatawala naye

Wakristo waaminifu watatawala pamoja na Kristo siku zijazo. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/*_tw/kt.html#faithful)

Mifano muhimu ya usemi katika sura hii

Mifano

Katika sura hii, Paulo anatumia mifano nyingi kufundisha maisha ya kikristo. Anatumia mifano ya mwanajeshi, mwanariadha na mkulima. Baadaye anatumia mifano ya aina nyingi ya vyombo vya nyumbani.

<< | >>

2 Timothy 2:1

Kuunganisha Maelezo

Paulo alipigapicha maisha ya Kikristo ya Timotheo kama maisha ya askari, kama maisha ya wakulima, kama maisha ya mwanamichezo

kuimarishwa katika neema iliyo katika Kristo Yesu

Maana inawezekana ni 1) 'basi Mungu kutumia neema akawapa kwenu katika Kristo Yesu kuwafanya kuwa imara (UDB) au 2) 'kuhamasisha mwenyewe, wakijua kwamba Mungu amewapa ninyi neema ambayo huja tu kwa njia ya Kristo Yesu

kati ya mashahidi wengi

"na mashahidi wengi kuna kukubaliana kwamba maneno yangu ni kweli"

mwaminifu

"kuaminika"

mwanangu

Paulo anamuona Timotheo kama mtoto wake kwa kuwa alimfundisha Timotheo kumwamini Kristo. "aliye kama mtoto wangu"

uyakabidhi kwa watu waaminifu

Paulo anatoa maelekezo kwa Timotheo kuwa ayakabidhi kwa watu waaminifu ili wayatumie kwa usahihi. "wafundishe"

2 Timothy 2:3

Shiriki mateso nami

Maana inawezekana ni 1) 'kuvumilia mateso kama mimi' (UDB) au 2) 'kushiriki katika mateso yangu'

Hakuna askari atumikae wakati akijihusisha na shughuli za maisha haya

"Hakuna askari atumikae wakati yeye hushiriki katika shuughuli ya kila siku ya maisha haya" au 'Wakati askari wanatumikia, hawana kupata mambo ya kawaida ambayo watu kufanya" watumishi wa Kristo lazima wasiruhusu maisha ya kila siku kuwaweka kutoka kufanya kazi kwa Kristo

Kama askari mzuri wa Kristo Yesu

Paulo anayafananisha mateso kwa ajili ya Kristo Yesu na mateso anayoyavumilia askari mzuri"

Afisa mkuu

"mmoja wapo aliyempendekeza yeye kama askari

mwanamichezo.... si taji isipokuwa awe ameshindana kwa sheria

watumishi wa Kristo inahitajika kufanya kile ambacho Kristo anasema kifanyike.

yeye sio taji isipokuwa awe ameshindana kwa sheria

"Wao watamvika taji yeye kama mshindi pekee ikiwa ameshindana kwa sheria

yeye hatapewa taji

"yeye hakusinda tuzo"

Kushinda kwa sheria

"Inashindana kwa mujibu wa sheria" au "madhubuti kumt'ii sheria"

wakati huo huo akijihusisha

Paulo anazungumzia uharibifu huu kama vile mtego unaowatega watu wakiwa wanatembea.

2 Timothy 2:6

Mkulima mwenye bidii apokee ujira wa mazao yake kwanza

Huu ni mfano wa tatu kwamba Paulo anampa Timotheo, msomaji anapaswa kuelewa kuwa watumishi wa Kristo wanahitaji kufanya kazi kwa bidii.

Fikiria juu ya ninachosema

Paulo alimpa Timotheo neno la picha, lakini hakuweza kabisa kuelezea maana zake, Yeye anatarajia Timotheo kufikiri nini alikuwa akisema kuhusu watumishi wa Kristo.

kwa maana Bwana

kwa sababu Bwana

Kwa kila kitu

"kuhusu vitu vyote"

2 Timothy 2:8

Kuunganisha maelezo

Paulo anatoa maelekezo Timothy juu ya jinsi ya kuishi kwa ajili ya Kristo, jinsi ya kuteseka kwa ajili ya Kristo, na jinsi ya kuwafundisha wengine kuishi kwa ajili ya Kristo.

kulingana na ujumbe wangu wa injili

kama ujumbe wangu wa injili usemavyo

ambavyo mimi nateseka

"kwa ambavyo mimi nateseka

hata kufungwa minyororo

"Kufungwa" inamaanisha kuwa gerezani.

Neno la Mungu haliwezi kulifungwi minyororo

"si vikwazo" au "si kufungwa" "ana uhuru kamili"

kwa wale ambao wamechaguliwa

"kwa watua ambao Mungu amewachagua"

wapate wokovu

"watapokea wokovu"

Utukufu wa milele

"Wanamtukuza Mungu milele" au "akizungumzia watu kwa Mungu milele"

Toka kwa uzao wa Daudi

"uzao" linamaanisha kizazi. "Ambao ni kizazi cha Daudi"

ambaye alifufuliwa kutoka kwa wafu

"Ambaye Mungu alimfufua"

2 Timothy 2:11

Msemo huu

"maneno haya"

Kufa

Hapa hii ina maana mtu kufa kwa nafsi yake. Kwa maneno mengine, kukataa kutoka katika tamaa yake mwenyewe.

tusipokuwa waaminifu

"hatakama tunamkosea Mungu" au "hatakama hatuwezi kufanya nini tunaamini Mungu anataka tufanye"

Yeye hawezi kujikana mwenyewe

"Yeye lazima daima hutenda kulingana na tabia yake" au "hawezi kutenda katika njia ambazo ni kinyume cha tabia yake halisi"

Ikiwa tumekufa pamoja naye ... hawezi kujikana mwenyewe

Hii ni kama wimbo au shairi ambalo Paulo ananukuu. Kama kwenye lugha yako kuna namna ya kuielezea kama shairi unaweza kutumia hapa. Kama hamna unaweza kutafsiri kama sentensi na sio shairi.

2 Timothy 2:14

maelezo ya jumla

Neno "ninyi" linaweza kuwa na maana ya 1) "Waalimu" (UDB) au 2) "watu wa Kanisa"

mbele za Mungu

'Katika uwepo wa Mungu' au 'wakijua kwamba Mungu hukuangalia wewe na hao'

si kwa ugomvi kuhusu maneno

"Si kujadiliana juu ya nini maana ya maneno" au "si kusema maneno ambayo kusababisha mapigano" au "si kusema maneno yenye maana ya kuumiza wengine"

haufai kitu

"hakuna yoyote mzuri" au "asiye na maana"

yanaangamiza

picha ni ya uharibifu wa jengo hilo. Wale ambao husikia ugomvi kuacha kuheshimu ujumbe wa Kikristo

kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu

"kujionyesha kwa Mungu kama mtu umeonyesha kuwa unastahili"

kama mfanyakazi

"Kama mfanyakazi" au "kama mfanyakazi"

utunzaji kwa usahihi

usahihi kuelezea

2 Timothy 2:16

Neno lao kuenea kama donda ndugu

"Nini wanasema yataendelea kusambaa kama ugonjwa wa kuambukiza" Kama vile donda ndugu kuenea katika mwili wa mtu na kuuteketeza, nini watu hao walikuwa wakisema ingeweza kuenea kutoka mtu hadi mtu na kudhuru imani ya wale ambao walisikia maneno hayo, "neno lao kuenea haraka na kusababisha uharibifu kama donda ndugu" au "Watu haraka kusikia wanayoyasema na kuwa wanaathirika nayo

Donda ndugu

wafu, huozo mwili. njia pekee ya kuweka donda ndugu kueneza na kumuua mtu mgonjwa ni kwa kukatwa eneo lililoathirika.

ufufuo ulishafanyika

Mungu tayari amewafufa waumini waliokufa kwenye uzima wa milele '

kubadirisha imani ya watu wengine

Kufanya baadhi ya waumini kuwa na shaka' au "kushawishi baadhi ya waumini kwa kuacha kuamini"

ambayo huongoza kwa zaidi na zaidi ya uasi

"inayoweza kusababisha watu wakawa kinyume na Mungu"

Himenayo na Fileto

Haya ni majina ya wanaume.

walioukosa ukweli

Paulo anazungumzia ukweli kama lengo kuu. Paulo anamaanisha watu hawa hawajaelewa ukweli na wanafundisha uongo.

2 Timothy 2:19

Msingi wa Mungu

Maana inawezekana ni 1) "Kanisa la Mungu limejenga tangu mwanzo" au 2) "ukweli juu ya Mungu" (UDB) au 3) "uaminifu wa Mungu."

anaetaja jina la Bwana

ambaye anasema yeye ni muumini katika Kristo

Aachane na uovu

Maana inawezekana ni 1)"kuacha kuwa mbaya" au 2) "kuacha kufanya mambo yasiyofaa.'"

Vyombo

Hii ni neno la ujumla kwa bakuli, sahani, sufuria, ambayo watu kuweka chakula au kinywaji humo. Kama lugha yako haina neno la ujumla, kutumia neno kwa 'bakuli' au 'sufuria.' Ni mfano kwa ajili ya watu

Heshima.... kutokuheshimu

Maana inawezekana ni 1) 'hafla maalum ... kawaida mara' (UDB) au 2) 'aina ya shughuli watu wema kufanya hadharani ... aina ya shughuli watu wema kufanya binafsi.'

ajitakase mwenyewe kutoka matumizi yasiyo ya heshima

Maana inawezekana ni 1) 'kujitenganisha mwenyewe kutoka kwa watu wasioheshimika" au 2) 'anayejifanya safi.'

chombo cha hesima

Muhimu kwa ajili ya hafla maarumu" au " muhimu kwa ajili ya shughuli watu wema kufanya kwa wazi"

Maelezo ya jumla

Kama vile chombo chenye thamani kinavyoweza kutumika kwa njia za heshima katika nyumba yenye utajiri, mtu yeyote atakayemrudia Mungu atatumika kwa heshima katika kufanya kazi njema.

Ametengwa maalumu, mwenye manufaa kwa Bwana, na ameandaliwa kwa kila kazi njema.

"Bwana amemtenga na yupo tayari kutumiwa na Bwana kufanya kazi njema.

Ametengwa

Hajatengwa kimwili lakini katika kutimiza kusudi.

2 Timothy 2:22

Kimbieni tamaa za ujana

Mafumbo haya yanamaanisha mbio haraka uwezavyo. Kukimbia ni kukimbia kitu kitakachoweza kuwadhuru ninyi, kufuata ni kukimbia kuelekea kitu ambacho kitakufanyia mema.

ukafuate haki

"kuitafuta haki"

Na

Maana inawezekana ni 1) Paulo alimtaka Timotheo kujiunga na wakristo wengine katika kutafuta haki' au 2) Paulo alimtaka Timotheo awe na amani na sio kugombana na waamini wengine.

nao wamwitao Bwana

"Wakristo" au "wote ambao wanaojiita watu wa Mungu"

kwa moyo safi

"Kwa nia ya dhati" au "kwa sababu nzuri"

ukatae upumbavu na maswali ya kipuuzi

"Kukataa kujibu maswali ya upumbavu" na "maswali ya kipuuzi"

Moyo safi

Paulo anazungumza juu ya sababu nzuri za kufanya jambo toka moyoni.

Huzaa ugonvi

Paulo anazungumza juu ya maswali ya kipuuzi akiyafananisha na mwanamke anayezaa mtoto. "inasababisha ugonvi"

2 Timothy 2:24

katika upole

"Kondoo" au "upole"

elimisha

"Elekeza" au "mafundisho" au "kurekebisha"

kuwapatia toba

"Kuwasaidia kuiacha dhambi yao"

kwa ujuzi wa ile kweli

"Ili waweze kuujua ukweli"

wanaweza kurejesha fahamu zao"

"wanaweza tena kufikiri mawazo mabaya" au "wanaweza kuanza kusikiliza Mungu tena"

mtego wa Shetani

Hii ni mfano kwa ajili ya watu ambao wanadhani wao ni kufuatia Mungu wakati wao ni kweli zifuatazo shetani.

wametekwa na yeye kwa ajili ya mapenzi yake

"Ambaye aliwateka wao na sasa amewafanya kufanya chochote anachotaka wafanye'

2 Timothy 3

2 Timotheo 03 Maelezo kwa jumla

Muundo na Mpangilio

"Siku za mwisho" inaweza kuwa na maana ya hapo mbeleni kabla ya Kristo kurudi. Kwa hivyo Paulo anatabiri katika mistari 1-9 na 13 kuhusu siku hizo. "Siku za mwisho" pia inaeza maanisha kipindi cha Ukristo (pamoja na wakati wa Paulo).Kwa hivyo anayofundisha Paulo kuhusu mateso yanahusu Wakristo wote. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/*_tw/kt.html#prophet and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/*_tw/kt.html#lastday)

<< | >>

2 Timothy 3:1

Sentensi Unganishi.

Paulo anataka Timotheo ajue ya kuwa katika siku za mwisho watu wataikataa kweri na mateso yatakuja, lakini katika hayo anaweza akalitumaini na kulitegemea andiko takatifu la Mungu.

Nyakati za Hatari.

Hizi zitakuwa ni siku, miezi na hata miaka ambayo Wakristo watakuwa katika hatari.

Wenye kujipenda wenyewe.

Matumizi ya neno "wenyekujipenda" inamaanisha upendo wa kiundugu au upendo wakiurafiki au watu wa familia moja, upendo wa asili kati ya marafiki na Jamaa(ndugu zao). Huu sio ya upendo utokao kwa Mungu.

Wenye majivuno.

Mtu yeyote mwenye kujisemea yeye katika hali ya kujisifu.

Wasiokuwa na Moyo wa kupenda.

"Wasiowapenda wa kwao( familia zao)

Wasio suluhishika

"Wasiokubaliana na mtu yeyote" au " wasio penda kusihi kwa amani na mtu yeyote".

Wasingiziaji.

"Washitaki wa uongo"

Wakali(wenye hasira)

"Katili" au " Mkali" au "watakuwa wakifanya mambo ili kuwaumiza wengine".

Wasiopenda Mema.

" Wenye kuchukia Mema"

Wakaidi.

"asiejali"( mtu wa kijiendea)

Majivuno( wenye viburi)

"Wakifikiri kuwa wao ni bora zaidi kuliko"

Siku za mwisho

Hii inamaanisha kuwa "anazungumzia siku za mbeleni baada ya Nyakati za Paulo. "Baadae kabla ya kurudi kwa Yesu"

2 Timothy 3:5

kuwa kama wacha Mungu

"Onekana kama wapenda dini au onekana kama wenye haki" au "Onekana kama watu wema"

Wataikana nguvu yake.

" Inamaana ya kuwa 1) "Wataikataa na wala hawataikubali nguvu ambayo Mungu alitaka kuwapatia" au 2) " Maisha yao hayataonesha udhibitisho wa ki Mungu kama wanavyodai".

Kutoka kwenye welekeo sahihi

" Kuepuka"

Watakao ingia kwenye familia

"Wakiingi katika nyumba na kushawishi sana"

Wanawake wapumbavu

"Wanawake ambao ni wachanga kiroho". Hii inaweza kuwa kwa sababu wanashidwa kutulia au kwa sababu hawana kazi au kwa sababu wamejawa na dhambi".

Waliojawa na dhaambi.

Maana zake ni 1) " Waliojawa na mizgo ya dhambi" au 2) " wanaotenda dhambi kila mara". Dhana kuu au wazo ni kwamba, hawawezi kuepukana na kutenda dhambi.

Wanaoongozwa na tamaa za kila aina.

Wanawake hawa hutamani vitu vingi kana kwamba wanaacha kumwabudu Kristo" au " Wanawake hawa wanaacha kumwabudu Kristo na badala yake wanaviendea vitu vingine wavitamanivyo."

2 Timothy 3:8

Yanne na Yambre

Majina haya mawili yanapatikana kwenye Biblia tu. Moja ya Mila inawaita kama waganga wa Misri waliokuwa wakimpinga Musa katika kitabu cha Kutoka 7-8.

Walisimama Kinyume

" Kupinga"

Sentensi unganishi

Paulo anawapa mfano wa walimu wawili wa uongo toka nyakati za Musa na kuonyesha namna watu watakavyokuwa. Anamsisitiza Timotheo kufuata mfano wa Paulo na kukaa katika neno la Mungu.

wako kinyume na kweli

"wanapinga injili ya Yesu"

Wamepotoka akili zao

"Hawawezi kufikiri kwa usahihi tena"

Kuendelea

" Kusonga mbele/ kupiga hatua"

Upumbavu

"Kutokuwa na uelewa" au " Upuuzi"

Dhahiri

"kuonekana wazi" au "kueleweka wazi"

Wasiokubalika kutokana na imani

Wanajaribiwa ni kwa namna gani wanamwamini Kristo na kumtii yeye na wakashindwa jaribu hilo. "bila imani ya kweli" au "wamethibitisha kuwa imani yao sio thabiti"

2 Timothy 3:10

wewe umeyafuata mafundisho yangu

" Lakini kwa wewe umekuwa makini katika kuyaangalia/kuyaenenda."

Mafundisho

"Maelekezo"

Mwenendo mzuri.

" Namna ya maisha"

Mateso ya mda

"kuwa na uvumilivu na watu"

Uvumulivu

Maana zake ni 1) "Nitaendelea kumtumikia Mungu hata katika hali ngumu ya kutoweza" au 2) " Nitaendelea kuenenda katika njia ya haki hata katika nyakati ngumu."

Walaghai/Watapeli

"Watu ambao huwadanganya watu kuhusu wao wenyewe" au " Watu ambao hujiweka tofauti na uhalisia wa maisha yao ya kweli."

Na katika hayo yote Bwana akaniokoa

Paulo anazungumzia namna ambavyo Bwana alimuokoa alipokuwa anateseka na hali ngumu na hatari.

kuishi katika maisha ya kumcha Mungu katika Kristo Yesu

"kuishi maisha ya kumcha Mungu kama mfuasi wa Yesu"

watateswa

"yawapaswa kuvumilia mateso"

watazidi kuwa waovu zaidi

"watakuwa waovu zaidi"

Watawapotosha wengine

"Watawasababisha watu wasimtii Kristo"

Wao wenyewe wamepotoshwa.

"Na watu wengine wawasababisha wasimtii Kristo"

2 Timothy 3:14

Endelea katika mambo ambayo umejifunza

" Usisahau yale uliyojifunza"

Maandiko matakatifu yatakayoweza kukufanya mtu mwenye hekima.

"Neno la Mungu linakupa Hekima utayoitaka"

2 Timothy 3:16

Kila andiko limeandikwa kwa uwezo wa Mungu

"Mungu aliyanena Maandiko yote kwa roho yake" au " Kila andiko ni pumzi ya Mungu", na kutolewa na roho wa Mungu. Mungu aliwambia watu nini waandike.

Lafaa.

"yenye kutumika" au " yenye faida"

Kuonya.

"kuonesha makosa"

Kurekebisha

"Kusahihisha makosa"

Kufundisha.

"kuwa mwenye maadili" au "kuleta katika uwezo wa kufanya kitu.

Mwenye uwezo dhabiti.

"Kuwa kamili"

mtu wa Mungu

Hii inamaana ya mtu yeyote anayemwamini Mungu awe mwanaume au mwanamke.

2 Timothy 4

2 Timotheo 04 Maelezo kwa jumla

Muundo na mpangilio

"Napeana amri hii ya dhati"

Paulo anapeana mashauri ya kibinafsi kwa Timotheo

Dhana Muhimu katika Sura hii

Taji

Maandiko matakatifu yanatumia aina nyingi ya mataji kama mfano wa vitu vingi. Inaonekana Kristo atawatuza waumini wake kama taji la kuishi maisha mazuri

__<< | __

2 Timothy 4:1

Sentensi unganishi.

Paulo aliendelea kumkumbusha Timotheo awe mwaminifu na kwamba Paulo yuko tayari kufa

Agizo lenye uzito

"Agizo la muhimu"

Mbele za Mungu na ya Kristo Yesu

"katika uwepo wa Mungu na Kristo Yesu"

walio hai na wafu

"walio hai na wafu" imetumika hapa kuwaelezea watu wote. "Watu wote waliowai kuishi"

kwa sababu ya kufunuliwa kwake na Ufalme wake

"Ufalme" inasimama kuonesha utawala wa Kristo kama Mfalme. "Atakaporejea kutawala kama mfalme"

Neno

"Neno" linamaanisha ujumbe. "Ujumbe kuhusu Kristo"

Usiofaa

"muda usiofaa"

Waambie watu dhambi zao

Kuwaambia watu makosa yao" au "kuwaambia watu kuwa walichofanya ni makosa"

himiza, kwa uvumilivu wote na mafundisho

"himiza na kufundisha watu na kuwa mvumilivu juu yao"

2 Timothy 4:3

kwa maana wakati unakuja

"kwasababu kwa muda fulani baadaya"

watu

Hali inaonyesha kuwa wale walikuwa watu wa kanisani

hawatachukuliana na mafundisho ya kweli

Hii ina maana kwamba mafundisho ambayo kanisa zima kuchukulia kuwa kweli na sahihi.

watajitafutia waalimu wa kufundisha kile wanacho kitamani, masikio yao yatakuwa tayari kusikia kile wakipendacho.

Maana inawezekana ikawa ni 1) kwa sababu ya tamaa zao binafsi, wao watajikusanyia karibu walimu ambao watasema nini wanataka kusikia au 2) kukusanya karibu walimu ambao wanakubaliana na tamaa zao binafsi na watasema nini wanataka kusikia.

masikio yao yatakuwa yametekenywa

Hii inamaanisha kuwa watu watafurahia kusikiliza mafundisho mapya na ya tofauti. "Kwa namna hii watatafta mambo mapya na ya tofauti ya kujifunza"

Wataacha kusikiliza mafundisho ya kweli

Paulo anazungumzia watu ambao hawajali tena na wala hawasikii. "hawasikilizi tena ukweli"

kazi ya uinjilisti

Hii ina maana kuwaambia watu kuhusu Yesu ni nani?alifanya nini kwaajili yao? na ni kwa jinsi gani waishi kwa ajili yake?

Watageukia hadithi

Paulo anazungumza na watu ambao wameanza kusikiliza hadithi. "wataanza kusikiliza hadithi ambazo si za kweli"

uwe mwaminifu

Paulo anataka wasikilizaji wake kuwa na fikra sahihi kwa kila jambo na aliwaambia wakitaka kuwa waaminifu wasitumie kileo.

2 Timothy 4:6

muda wa kuondoka kwangu umewadia

"Karibuni nitakufa na kuiacha dunia hii", Paulo alitambua kuwa hataishi kwa muda mrefu.

Nimeshindana katika mashindano mema

Hii ni michezo mfano wa mapigano, kumenyana, au ndondi. Paul amefanya kwa nguvu zake zote. Hii pia inaweza kutafsiriwa kama "Nimefanya kwa uwezo wote" au "Nilijitoa kwa nguvu zangu zote."

mwendo nimeumaliza

Picha hii inaashiria kumaliza maisha kama kufikia mstari wa kumalizia mbio. "Mimi nimemalize kile ninachohitajika kufanya."

imani nimeilinda

Maana inawezekana ikawa ni 1) "niimezishika mafundisho kuhusu nini tunaamini mbali na kila aina ya upotofu" au 2) "Nimekuwa mwaminifu katika kufanya huduma yangu"

Taji ya haki imewekwa kwa ajili yangu

"nitapewa taji ya haki'

Taji ya haki

Maana inaweze kuwa i 1) taji ni tuzo ambayo Mungu huwapa watu ambao wamekuwa wakiishi kwa njia sahihi au 2) taji ni mfano kwa ajili ya haki. Kama ambavyo hakimu wa mbio inatoa taji kwa mshindi, Paulo atakapomaliza maisha yake, Mungu atamtangaza kwamba Paulo ni mwenye haki.

taji

ni shada iliyotengenezwa kwa majani ya mti (laurel) ambayo ilitolewa kwa washindi wa mashindano ya riadha

siku ile

"siku ambayo Bwana atarudi tena" au "kwa siku ile Mungu atakapo wahukumu watu"

tayari nimekwisha kumiminwa

Paulo anazungumzia utayari wake wa kufa akijifananisha na kikombe cha mvinyo kilivyo tayari kumiminwa kama sadaka kwa Mungu.

bali pia kwa wote wanaongojea kwa shauku kuonekana kwake.

Hii inaweza kuelezewa kama tukio la wakati ujao. "lakini pia atawapa wale wangojao kwa shauku kurudi kwake"

2 Timothy 4:9

Sentensi unganishi

Katika kufunga kwake, Paul alimtia moyo Timotheo aje kwake, anamuambia amlete Luka, anataja baadhi ya watu ambao wamejitenga na Bwana, na anatoa salamu kwa wenyeji wa pale pamoja na Timotheo.

kwa haraka

"mapema iwezekanavyo"

kwani

kwasababu

dunia ya sasa

Maana inaweze ikana ni 1) mambo ya muda ya dunia hii, "raha na faraja ya dunia hii," au 2) hii maisha ya sasa na salama kutokana na kufa. Huenda Dema alikuwa na hofu kwamba watu wangeweza kumuua kama atakaa pamoja na Paulo.

Kreske alikwenda ......na Tito alikwenda

Watu hawa wawili waliondoka na kumuacha Paul, lakini Paulo hasemi kwamba wao pia "waliupenda ulimwengu huu wa sasa" kama Dema.

Dema ... Kreseni ... Tito

Haya ni majina ya wanaume.

Dalmatia.

Hili ni jina la mkoa

2 Timothy 4:11

yeye ni muhimu kwangu katika kazi hii

Maana inaweza ikawa ni 1) "anaweza kunisaidia katika huduma" au 2) "anaweza kunisaidia kwa kunihudumia mimi".

joho

Vazi zito linalovaliwa juu ya nguo

Karpo

Hili ni jina la mwanaume.

Vitabu

Hii inamaanisha "gombo" Hii ni aina ya kitabu kinachoandikwa kwenye ngozi. Baada ya kuandika au kusoma gombo hukunjwa kwa kutumia fimbo mwishoni.

Gombo dogo

Hii ni aina ya gombo. Hizi huwa zinatengenezwa kwa kutumia ngozi za wanyama"

2 Timothy 4:14

alinitendea maovu mengi

"alitenda maovu dhizi yangu" au "alinitendea mambo mabaya "

Bwana atamlipa kulingana na matendo yake

"Bwana atamuadhibu kutokana na aliyoyafanya"

yeye, yake

Yote haya yanamaanisha Alexanda

yeye alilipinga sana line neno letu

"Alipinga kwa jitihada kubwa ujumbe wetu" au "yeye alipinga sana maneno yetu"

hakuna mtu yeyote aliyesimama nami, badala yake wote waliniacha

"hakuna aliyekaa na mimi na kunisaidia, badala yake , kila mmoja aliondoka"

Tendo hilo lisihesabiwe dhidi yao

"mimi sitaki Mungu awaadhibu wale waumini kwa kuniacha mimi"

Alekizanda

Hili ni jina la mwanaume.

Mfua vyuma

"anayefanya kazi ya kutengeneza vyuma"

2 Timothy 4:17

alisimama pamoja nami

"alisimama pamoja nami kunisaidia mimi"

neno linenwe kwa ukamilifu na mataifa wapate kusikia

Maana inaweze kuwa ni 1) hii ilikuwa tayari kimeshatokea au 2) hii ilikuwa bado katika siku zijazo kwa ajili ya Paulo, "ili niweze kusema neno lake kikamilifu na hivyo watu wa mataifa yote wapate kusikia."

Niliokolewa katika kinywa cha simba

Hatari hii inaweza kuwa ni ya kimwili, kiroho, au vyote viwili. Mimi niliokolewa kutoka hatari kubwa."

2 Timothy 4:19

nyumba ya Onesiforo

"nyumba" inasimama kuelezea watu wanaoishi pale. "familia ya Onesiforo"

Onesiforo

Hili ni jina la mwanaume.

Erasto, Trifimo, Eubulo, Pude, Lino

Haya ni majina ya wamaume.

Mileto

Hili ni jina la mji uliopo kusini kwa Efeso.

Fanya hima uje

"tengeneza njia uje"

kabla ya kipindi cha baridi

"kabla ya kipindi cha baridi"

Pude, Lino, Claudia na ndugu wote

"Pude, Lino, Claudia na ndugu wote wanawasalimia"

Claudia

Hili ni jina la mwanamke.

Ndugu wote

"ndugu" inmaanisha waamini wote wanaume na wanawake.

Mungu awe pamoja na roho yako

"Naomba kwamba Mungu aifanye roho yako kuwa imara"

Neema iwe nanyi

"Naomba kwamba Bwana aoneshe rehema zake kwenu"

Neema

"huruma yake" au "upendeleo wake"