Kiswahili: translationNotes Print

Updated ? hours ago # views See on WACS

Utangulizi wa 3 Yohana

Sehemu ya 1: Utangulizi wa Ujumla

Maelezo ya Kitabu cha 3 Yohana

  1. Utangulizi (1:1)
  2. Kutia moyo na maelekezo ya kuonyesha ukarimu (1:2-8)
  3. Diotrefe na Demetrio (1:9-12)
  4. Hitimisho (1:13-14)

Nani aliandika Kitabu cha 3 Yohana?

Barua haina jina la mwandishi. Mwandishi alijitambulisha mwenyewe kama "mzee" (1:1). Barua hii pengine ilikuwa imeandikwa na Mtume Yohana alipokaribia kuaga dunia.

Je, kitabu cha 3 Yohana kinahusu nini?

Yohana aliandika barua hii kwa muumini mmoja aitwaye Gayo. Alimwambia Gayo awe na ukarimu kwa waumini wenzake ambao walikuwa wakisafiri kupitia eneo lake.

Je, kichwa cha kitabu hiki kinapaswa kutafsiriwaje?

Watafsiri wanaweza kuchagua kuita kitabu hiki kwa kichwa chake cha jadi, "3 Yohana" au "Yohana wa Tatu." Au wanaweza kuchagua kichwa cha wazi, kama "Barua ya Tatu Kutoka kwa Yohana" au "Barua ya Tatu Aliyoandika Yohana." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/*_tm/translate.html#translate-names)

Sehemu ya 2: Dhana muhimu za Kidini na za Kitamaduni

Je, ukarimu ni nini?

Ukarimu ulikuwa dhana muhimu katika Mashariki ya Karibu ya kale. Ilikuwa muhimu kuwa na urafiki kwa wageni au watu wasio wa eneo hilo na kutoa msaada kwao ikiwa wangehitaji. Katika 2 Yohana, Yohana aliwakataza Wakristo kutowaonyesha ukarimu walimu wa uongo. Katika Yohana 3, Yohana aliwahimiza Wakristo kuonyesha ukarimu wageni waaminifu.

Sehemu ya 3: Masuala muhimu ya Tafsiri

Je! Mwandishi hutumuia namuna gani uhusiano wa familia katika barua yake?

Mwandishi alitumia maneno "ndugu" na "watoto" kwa namna ambayo inaweza "inaweza kuleta tatizo. Maandiko mara nyingi hutumia neno "ndugu" kutaja Wayahudi. Lakini katika barua hii, Yohana alitumia neno kuelezea Wakristo. Pia, Yohana aliwaita waumini wengine "watoto" wake. Hawa ni waumini aliowafundisha kumtii Kristo.

Yohana pia alitumia neno "Myunani" kwa njia ambayo inaweza inaweza kuleta tatizo. Maandiko mara nyingi hutumia neno "Myunani" kuwataja watu ambao si Wayahudi. Lakini katika barua hii, Yohana alitumia neno kutaja wale ambao hawakuamini Yesu.

3 John 1

3 John 1:1

Sentensi unganishi

Yohana anatuma salaam kwa Gayo

Maelezo ya jumla

Hii ni barua mtu binafsi Yohana anaituma kwa Gayo. Maneno yote ya kiwakilishi cha majina yanamtaja Gayo katika umoja.

Mzee

Ni kiwakilishi cha Yohana, mtume na mwanafunzi wa Yesu. Yeye mwenyewe anajiwakilisha kama "mzee" pengine kwa sababu ya umri wake au kwasababu ya uongozi wake wa kanisa. Jina la mwandishi linaweza kufupishwa: Mimi, Yohana mzee, ninaye andika.

Gayo

Huyu ni mshirika mwamini ambaye Yohana anamwandikia barua hii.

Ambaye ninayempenda katika kweli

"Ambaye ninampenda kweli"

Unaweza kufanikiwa katika mambo yote na kuwa na afya

"Unaweza kufanya mambo yote vizuri na kuwa na afya"

Kama na roho yako ifanikiwavyo

"Kama vile unavyoendelea vizuri kiroho"

Ndugu

"washirika waumini"

dhihirisha ushuhuda wa kweli yako, kuwa unatembea katika kweli

"aniambia kuwa unaishi kulingana na ukweli wa Mungu"

Wanangu

Yohana anazungumzia wale aliowafundisha kumwamini Yesu kama vile watoto wake. Hii inauelezea upendo wake na nia yake kwa ajili yao. Inaweza pia kuwa yeye mwenyewe aliwaongoza kumjua Bwana. "Watoto wangu wa kiroho"

3 John 1:5

Sentensi unganishi

Kusudi la Yohana la kuandika barua hii ilikuwa kumhimiza Gayo kuwa makini katika njia aliyoianza ya kufundisha Biblia; kisha anazungumzia habari za watu wawili, mmoja mwovu na mwingine mwema.

Maelezo ya Jumla

Hapa neno "sisi" linamtambulisha Yohana na wale waliokuwa pamoja naye na yawezekana linawaunganisha waumini wote.

Mpendwa

Hapa inatumika kama neno la utambulisho kwa wafuasi waumini.

Unaenenda kwa uaminifu

"Unatenda kwa uaminifu kwa Mungu" au "Umekuwa mtii kwa Mungu"

unapowahudumia ndugu na wageni

"Kuhudumia ndugu waumini na wale usiowajua"

ambao wametoa ushuhuda wa upendo wako mbele ya kanisa.

"Wageni, ambao wamewaambia waumini katika kanisa jinsi mnavyowapenda"

Unafanya vizuri kuwasafirisha

"Kwa unyenyekevu ninawaomba mpate kuwasafirisha

Kwa sababu kwa ajili ya Jina, walienda

Hapa Jina linamaanisha Yesu. Walienda kuwaambia watu wengine kuhusu Yesu.

bila kuchukua kitu chochote

Bila kupokea zawadi au misaada

wa Mataifa

Hapa watu "wa mataifa" Haimaanishi kuwa ni watu wasio Wayahudi. Inamaanisha watu wasio na tumaini kwa Yesu.

ili tuwe watenda kazi wenza kwa ajili ya kweli

"Ili kwamba tutashirikiana nao kuutangaza ukweli wa Mungu kwa watu"

3 John 1:9

Maelezo ya jumla

Neno "sisi" linamwelezea Yohana na wele waliokuwa pamoja naye bila kumjumuisha Gayo.

kusanyiko

Hapa anamtaja Gayo na kundi la waumini wanaokutana pamoja kumwabudu Mungu.

Diotrofe

Alikuwa hapo awali mmoja wa kundi la waumini waliokuwa wakikusanyika

anayependa kuwa wa kwanza miongoni mwao

"Aliyependa kuonekana kuwa wa muhimu sana miongoni mwao" au "ambaye alipenda kujifanya kama vile ni kiongozi wao"

jinsi anavyosema maneno mabaya dhidi yetu

"Jinsi anavyonena mambo mabaya kutuhusu sisi na hakika siyo ya kweli"

yeye mwenyewe

Neno "yeye mwenyewe" linamwelezea Diotrofe aliyekuwa akifanya mambo hayo.

hawapokei ndugu

hataki kuwapokea ndugu waumini"

Hata huwakataza wengine ambao wanatamani kuwakaribisha hao

"Anawazuia wale wanaotaka kuwakaribisha waumini"

na kuwafukuza watoke kwenye kusanyiko.

"Anawalazimisha kutoka kwenye kusanyiko"

3 John 1:11

Maelezo ya jumla

Hapa neno "sisi" linaelezea kuhusu Yohana na wale waliokuwa pamoja naye bila kumjumuisha Gayo.

Mpendwa

Hapa inatumika kama neno la utambulisho kwa wafuasi waumini.

usiige kilicho kibaya

"Usifuatishe mambo maovu ambayo watu wanayatenda"

bali iga kilicho chema

"Fuatisha mambo mema ambayo watu wanayatenda"

ni wa Mungu

"Yanatokana na Mungu"

hajamwona Mungu

eye si mali ya Mungu" au "Hajamwamini Mungu"

Demetrio ameshuhudiwa na wote

Wote ambao wanamfahamu Demetrio wanamshuhudia" au "Kila mwumini anayemjua Demetrio ananema mema kumhusu yeye"

Demetrio

Huyu yawezekana kuwa ni mtu ambaye Yohana anamtaka Gayo na kusanyiko lote kumkaribisha wakati wa ziara yake.

na kweli yenyewe

"Kweli yenyewe pekee inanena ukweli juu yake, kwamba ni mtu mwema"

sisi pia ni mashahidi

"Sisi pia tunanena mema yahusuyo Demetrio"

3 John 1:13

Maelezo ya jumla

Huu ni mwisho wa barua ya Yohana kwa Gayo. Anampatia mambo ya hitimisho na kuifunga kwa salaamu.

lakini sipendi kukuandikia kwa kalamu na wino

Yohana hana utashi wa kuwaandikia mambo mengine yote. Hasemi kwamba kwamba angewaandikia mambo fulani zaidi ya kalamu na wino.

ana kwa ana

"Kwa pamoja" au "kwa mmoja mmoja"

Amani iwe pamoja nawe

"Mungu aweza kukupa amani"

Marafiki wanakusalimu

"Marafiki hapa wanakusalimu

marafiki

"Rafiki zako" au "Waumini wenzako"