Genesis 1

Genesis 1:1

Hapo mwanzo, Mungu aliumba mbingu na nchi

"Hii inahusu jinsi gani Mungu aliumba mbingu na nchi hapo mwanzo." Kauli hii inafupisha sura iliyobaki. Lugha zingine huitafsiri kama "Hapo zamani sana Mungu aliziumba mbingu na nchi."

Hapo mwanzo

Hii inalenga kuanza kwa dunia na kila kitu ndani mwake.

mbingu na nchi

"anga, ardhi, na kila kitu ndani yao"

mbingu

Hapa inamaanisha anga

Bila umbo na tupu

Mungu alikuwa hajaweka dunia katika mpangilio.

vilindi

"maji" au "maji ya kina kirefu" au "maji mengi"

maji

"maji" au "uso wa maji"

Genesis 1:3

Na kuwe na nuru

Hii ni amri. Kwa kuamuru kuwepo na nuru, Mungu alifanya iwepo.

Mungu akaona nuru, kuwa ni njema

"Mungu aliifikiria nuru na kufurahishwa nayo." Hapa "Njema" inamaanisha "kufurahisha" au "inayofaa."

akaigawa nuru na giza

"alitenganisha nuru na giza" au "alifanya kuwepo na nuru wakati mmoja na giza wakati mwingine." Hii inamaanisha Mungu aliumba wakati wa mchana na usiku.

Ikawa jioni na asubuhi, siku ya kwanza

Mungu alifanya vitu hivi katika siku ya kwanza ambapo ulimwengu ulianza kuwepo.

jioni na asubuhi

Hii inamaanisha siku nzima. Mwandishi anazungumzia siku nzima kana kwamba ni sehemu mbili. Kwa tamaduni za Kiyahudi, siku moja huanza baada ya jua kuzama.

Genesis 1:6

Na kuwe na anga kati ya maji ...na ligawe

Hizi ni amri. Kwa kuamuru kwamba anga kati ya maji iwepo na igawe maji, Mungu alifanya iwepo na kugawa maji na maji.

anga

"anga tupu na wazi". Watu wa Kiyahudi walichukulia uwazi huu kuwa na umbo kama la kuba au bakuli lililofunikwa.

kati ya maji

"ndani ya maji"

Mungu alifanya anga na kugawanya maji

"kwa namna hii, Mungu alifanya anga na kugawa maji." Mungu alipozungumza, ilitokea. Sentensi hii inaeleza kitu gani Mungu alifanya alipokuwa akizungumza.

ikawa hivyo

"ilitokea kama hivyo" au "Hivyo ndivyo ilivyotokea". Mungu alichoamuru kilitokea kama alivyotamka kitokee. Msemo huu hujitokeza katika sura nzima na una maana ile ile kila unapojitokeza.

jioni na asubuhi

Hii inamaanisha siku nzima. Mwandishi anazungumzia siku nzima kana kwamba ni sehemu mbili. Kwa tamaduni za Kiyahudi, siku moja huanza baada ya jua kuzama.

siku ya pili

Hii inamaanisha siku ya pili ambapo ulimwengu ulipoanza kuwepo.

Genesis 1:9

Maji yaliyo chini ..yakusanyike

Hii inaweza kutafsiriwa kama kitenzi endelevu. Hii ni amri. Kwa kuamuru maji yakusanyike, Mungu aliyafanya yakusanyike pamoja.

na ardhi kavu ionekane

Maji yalikuwa yamefunika ardhi. Basi maji yalisogea pembeni na baadhi ya ardhi kubaki wazi. Hii ni amri. Kwa kuamuru kwamba ardhi kavu ionekane, Mungu alifanya ionekane. "na ardhi kavu ionekane" au "na ardhi kavu iwe wazi" au "na ardhi ifunuliwe"

ardhi kavu

Hii inamaanisha ardhi ambayo haijafunikwa kwa maji. Haimaanishi ardhi ambayo ni kavu sana kwa ajili ya kilimo.

ikawa hivyo

"ilitokea kama hivyo" au "Hivyo ndivyo ilivyotokea". Mungu alichoamuru kilitokea kama alivyotamka kitokee. Msemo huu hujitokeza katika sura nzima na una maana ile ile kila unapojitokeza.

nchi

"ardhi" au "chini"

Akaona kuwa ni vyema

Hapa "ni" inamaanisha nchi na bahari.

Genesis 1:11

Na nchi ichipushe mimea

Hii ni amri. Kwa kuamuru ya kwamba mimea ichipuke juu ya ardhi, Mungu alifanya ichipuke. "Mimea na ichipuke juu ya ardhi" au "Mimea na iote juu ya ardhi"

mimea: miche inayotoa mbegu na miti ya matunda izaayo matunda

"mimea, kila mche unaozaa mbegu na kila mti unaozaa matunda" au "mmea. Kuwe na mimea itoayo mbegu na matunda ya miti yazaayo matunda". Mimea hutumika hapa kama msemo wa jumla inaojumlsiha mimea na miti yote.

miche

Hii ni aina ya mimea ambayo ina mashina laini, na sio kama ya mbao

miti ya matunda izaayo matunda ambayo mbegu yake imo ndani yake

miti izaayo matunda yenye mbegu ndani yake

kila kitu kwa namna yake

Mbegu zingezaa mimea na miti ambayo ingekuwa kama zile zilipotokea. Kwa namna hii, mimea na miti zingejizalisha zenyewe.

ikawa hivyo

"ilitokea kama hivyo" au "Hivyo ndivyo ilivyotokea". Mungu alichoamuru kilitokea kama alivyotamka kitokee. Msemo huu hujitokeza katika sura nzima na una maana ile ile kila unapojitokeza.

Mungu akaona kuwa ni vyema

Hapa "ni" inamaanisha mimea, mazao na miti.

jioni na asubuhi

Hii inamaanisha siku nzima. Mwandishi anazungumzia siku nzima kana kwamba ni sehemu mbili. Kwa tamaduni za Kiyahudi, siku moja huanza baada ya jua kuzama.

siku ya tatu

Hii inamaanisha siku ya tatu ambapo ulimwengu ulianza kuwepo.

Genesis 1:14

Kuwe na mianga katika anga

Hii ni amri. Kwa kuamuru ya kwamba mianga iwepo, Mungu alifanya iwepo

mianga katika anga

"vitu ving'aavyo katika anga" au"vitu vitoavyo mwanga katika anga". Hii inaamanisha jua, mwezi na nyota

katika anga

"katika uwazi wa anga" au "katika uwazi mkubwa wa anga"

kutenganisha mchana na usiku

"kutenganisha mchana na usiku." Hii inamaanisha "kutusaidia kutambua tofauti kati ya mchana na usiku." Jua inamaanisha ni mchana, na mwezi na nyota humaanisha ni usiku.

na ziwe kama ishara

Hii ni amri. Kwa kuamuru ya kwamba ziwe kama ishara, Mungu alizifanya zitumike kama ishara. "Na zitumike kama ishara" au "na zioneshe"

ishara

Hapa inamaanisha kitu kinachofunua au kinacholenga jambo

majira

"Majira" inamaanisha nyakati zitakazotengwa kwa sikukuu na mambo mengine ambayo watu hufanya.

kwa majira, kwa siku na miaka

Jua, mwezi, na nyota huonyesha muendelezo wa muda. Hii inatusaidia kutambua ni wakati gani tukio hutokea kila wiki, mwezi au mwaka.

ziwe mianga katika anga ili kutoa mwanga juu ya nchi

Hii ni amri. Kwa kuamuru ziwe mianga juu ya nchi, Mungu alifanya zimulike juu ya nchi

kutoa mwanga juu ya nchi

"kutoa mwanga juu ya nchi" au "kuangazia nchi". Nchi haitoi mwanga yenyewe bali hupata mwanga na kurudisha mwanga.

ikawa hivyo

"ilitokea kama hivyo" au "Hivyo ndivyo ilivyotokea". Mungu alichoamuru kilitokea kama alivyotamka kitokee. Msemo huu hujitokeza katika sura nzima na una maana ile ile kila unapojitokeza.

Genesis 1:16

Mungu akafanya mianga mikuu miwili

"Kwa njia hii Mungu akafanya mianga miwili mikuu" Sentensi hii inaelezea Mungu alichofanya alipozungumza.

mianga miwili mikuu

"mianga miwili mikuu" au "mianga miwili ing'aaro". Mianga miwili mikuu ni jua na mwezi.

kutawala mchana

"kuongoza mchana kama mtawala angozapo kundi la watu" au "kuweka alama katika siku"

siku

Hii inamaanisha masaa ya mchana pekee

mwanga mdogo

"mwanga mdogo" au "mwanga hafifu"

katika anga

"katika mbingu" au "katika uwazi wa angani"

kutenganisha mwanga na giza

"kutenganisha mwanga na giza" au "kutoa mwanga kwa kipindi kimoja na giza kwa kingine.

Mungu akaona kuwa ni vyema

Hapa "ni" inamaanisha jua, mwezi na nyota.

jioni na asubuhi

Hii inamaanisha siku nzima. Mwandishi anazungumzia siku nzima kana kwamba ni sehemu mbili. Kwa tamaduni za Kiyahudi, siku moja huanza baada ya jua kuzama.

siku ya nne

Hii inamaanisha siku ya nne ambapo ulimwengu ulianza kuwepo.

Genesis 1:20

Na maji yajae idadi kubwa ya viumbe hai

Hii ni amri. Kwa kuamuru viumbe hai wajaze maji, Mungu alifanya viwepo. Baadhi ya lugha huweza kuwa na neno moja linalomaanisha aina wote wa samaki na viumbe wa baharini. "Maji yajae viumbe wote" au "viumbe wengi wanao ogelea waishi baharini".

na ndege waruke

Hii ni amri. Kwa kuamuru ya kwamba ndege waruke, Mungu alifanya waruke.

ndege

"wanyama warukao" au "vitu vinavyoruka"

anga tupu ya angani

"nafasi iliyo wazi ya angani" au "anga"

Mungu aliumba

"kwa njia hii Mungu aliumba"

viumbe wa majini wakubwa

"wanyama wakubwa wanaishi ndani ya bahari"

kwa aina yake

Vitu hai vya "aina" moja ni sawa na kule vilivyotokea.

kila ndege mwenye mabawa

"kila kitu kipaacho chenye mabawa." Iwapo neno kwa ajili ya ndege linatumika, linaweza kuwa kawaida kwa baadhi ya lugha kusema "kila ndege" kwa maana kila ndege ana mabawa.

Mungu akaona kuwa ni vyema

Hapa "ni" inamaanisha ndege na samaki.

Genesis 1:22

akavibariki

"alibariki wanyama aliowaumba"

zaeni na muongezeke

Hii ni baraka ya Mungu. Aliwaambia wanyama wa baharini kuzalisha wanyama wengine wa baharini kama wao wenyewe, ili kwamba wawe wengi baharini. Neno "ongezeka" linafafanua jinsi gani wanapaswa "kuongezeka"

ongezeka

"ongezeka kwa idadi kubwa" au "kuwa wengi"

Ndege waongezeke

Hii ni amri. Kwa kuamuru ya kwamba ndege waongezeke, Mungu aliwafanya ndege waongezeke.

ndege

"wanyama warukao" au "vitu virukavyo"

jioni na asubuhi

Hii inamaanisha siku nzima. Mwandishi anazungumzia siku nzima kana kwamba ni sehemu mbili. Kwa tamaduni za Kiyahudi, siku moja huanza baada ya jua kuzama.

siku ya tano

Hii inamaanisha siku ya nne ambapo ulimwengu ulianza kuwepo.

Genesis 1:24

nchi na itoe viumbe hai

"Nchi na itoe vitu hai" au "na viumbe hai vingi viishi juu ya nchi". Hii ni amri. Kwa kuamuru ya kwamba nchi itoe viumbe hai, Mungu alifanya nchi itoe viumbe hai.

kila kiumbe kwa aina yake

"ili kwamba kila aina ya mnyama izae aina yake zaidi"

mnyama wa kufugwa, vitu vitambaavyo, na wanyama wa nchi

Hii inaonyesha ya kwamba Mungu aliumba kila aina ya wanyama. Iwapo lugha yako inayo namna nyingine ya kuunganisha wanyama wote katika kundi, basi waweza tumia hilo neno, au tumia kundi hili.

mnyama wa kufugwa

"wanyama wanaotunzwa na binadamu"

vitu vitambaavyo

"wanyama wadogo"

wanyama wa nchi

"wanyama mwitu" au "wanyama hatari"

ikawa hivyo

"ilitokea kama hivyo" au "Hivyo ndivyo ilivyotokea". Mungu alichoamuru kilitokea kama alivyotamka kitokee. Msemo huu hujitokeza katika sura nzima na una maana ile ile kila unapojitokeza.

Mungu akafanya wanyama wa nchi

"Kwa njia hii Mungu aliwafanya wanyama wa nchi"

Akaona kuwa ni vyema

Hapa "ni" inamaanisha viumbe hai wa nchi.

Genesis 1:26

na tufanye

Hapa neno "tumfanye" lina maana ya Mungu. Mungu alisema alichokusudia kukifanya. Kiwakilishi nomino "tu" ni wingi. Uwezekano wa sababu za wingi ni 1) wingi huu unaweza maanisha Mungu anajadili jambo na malaika ambao hukamilisha baraza lake la mbinguni au 2) wingi huu unaonyesha dalili baadae katika Agano Jipya kuhusisha ya kwamba Mungu yupo katika Utatu Mtakatifu. Baadhi hutafsiri kama "Na nifanye" au "Nitafanya". Kama utafanya hivi, basi zingatia kuweka maandishi mafupi kusema kuwa neno lina wingi.

mtu

"binadamu" au "watu". Neno hili hapa halimaanishi jinsia ya kiume pekee.

katika mfano wetu, wa kufanana na sisi

Misemo hii miwili ina maana moja na inasisitiza kuwa Mungu alifanya binadamu awe kama yeye. Mstari huu hausemi ni kwa njia zipi Mungu alifanya watu wawe kama yeye. Mungu hana mwili, kwa hiyo haimanishi watu watafanana na Mungu. "na kufanana na sisi".

wawe na mamlaka juu ya

"kutawala" au "kuwa na mamlaka juu"

Mungu akamuumba mtu ...alimuumba

Sentensi hizi mbili zina maana moja na zinasisitiza ya kwamba Mungu aliumba watu katika mfano wake.

Mungu akamuumba mtu

Namna Mungu alivyoumba binadamu ni tofauti na jinsi alivyoumba vitu vingine vyote. Usieleze bayana ya kwamba aliumba binadamu kwa kuongea, kama mistari ya nyuma inavyoonyesha.

Genesis 1:28

Mungu akawabariki

Neno "akawabariki" lina maana ya mwanamume na mwanamke aliowaumba Mungu.

zaeni na kuongezeka

Mungu alimwambia mwanamume na mwanamke kuzalisha watu zaidi kama wao wenyewe ili kwamba wawe wengi kama wao. neno "kuongezeka" linaelezea namna wanavyotakiwa "kuzaa".

Jazeni nchi

jazeni nchi na watu.

Genesis 1:30

Taarifa ya jumla:

Mungu anaendelea kuzungumza

kila ndege wa angani

"ndege wote wanaopaa angani"

chenye pumzi ya uhai

"kinachopumua". Msemo huu unasisitiza ya kwamba wanyama hawa walikuwa na uhai tofauti na mimea. Mimea haiwezi kupumua, na ilipaswa kutumika kama chakula cha wanyama. Hapa "uhai" una maana ya uhai wa mwili.

ikawa hivyo

"ilitokea kama hivyo" au "Hivyo ndivyo ilivyotokea". Mungu alichoamuru kilitokea kama alivyotamka kitokee. Msemo huu hujitokeza katika sura nzima na una maana ile ile kila unapojitokeza.

Tazama

"hasa". Hapa neno "tazama" linaongeza msisitizo kwa kile kinachofuata.

kikawa chema sana

Mungu alipotazama kila kitu alichokiumba, "kikawa chema sana".

jioni na asubuhi

Hii inamaanisha siku nzima. Mwandishi anazungumzia siku nzima kana kwamba ni sehemu mbili. Kwa tamaduni za Kiyahudi, siku moja huanza baada ya jua kuzama.

siku ya sita

Hii inamaanisha siku ya sita ambapo ulimwengu ulianza kuwepo.

Genesis 2

Genesis 2:1

mbingu

"anga" au "mbingu"

na viumbe hai vyote vilivyo jaza

"na viumbe hai vingi ambavyo vimo ndani yao" au "na makundi ya viumbe hai vinavyoishi ndani mwao"

zilimalizika

Hii inaweza kutajwa katika njia endelevu "Mungu alimaliza kuviumba"

Siku ya saba Mungu alifikia mwisho wa kazi yake

Mungu hakufanya kazi kabisa katika siku ya saba.

alifikia mwisho wa

Hii ni lahaja. "alikuwa amemaliza"

alipumzika siku ya saba kutoka kwenye kazi yake yote

"katika siku hiyo hakufanya kazi"

Mungu akaibarikia siku ya saba

Yawezekana maana ni 1) Mungu alisababisha siku ya saba kutoa matokeo mazuri au 2) Mungu alisema ya kwamba siku ya saba ilikuwa nzuri.

na akaitakasa

"na akaiweka kando" au "na kuifanya iwe yake"

katika siku hiyo alipumzika kutoka kwenye kazi yake yote

"katika siku hiyo hakufanya kazi"

Genesis 2:4

Taarifa ya jumla

Sura ya pili iliyobaki ya Mwanzo inaelezea juu ya Mungu alivyoumba watu katika siku ya sita.

Haya yalikuwa ni matukio yahusuyo mbingu na nchi

"Hii ni habari ya mbingu na nchi" au "Hii ni simulizi ya mbingu na nchi" Yawezekana maana ni 1) ni kifupisho cha matukio yaliyoelezwa katika Mwanzo 1:1-2:3 au 2) inakaribisha matukio yaliyoelezwa katika Mwanzo 2.

vilipoumbwa

Yahwe Mungu aliviumba". Katika sura ya 1 mwandishi kila mara anamzungumzia Mungu kama "Mungu", lakini katika sura ya 2 kila mara anamzungumzia Mungu kama "Yahwe Mungu".

katika siku ambayo Yahwe Mungu aliumba

"Yahwe Mungu alipoumba". neno "siku" linamaana ya muda wote wa uumbaji na siyo siku hiyo moja pekee.

Yahwe

Hili ni jina la Mungu ambalo alilifunua kwa watu wake katika Agano la Kale.

Hapakuwa na msitu wa shambani

hapakuwa na vichaka vimeavyo msituni ambayo wanyama wangeweza kula

hapakuwa na mmea wa shambani

hapakuwa na mimea ya majani kama mboga au mboga za kijani ambazo wanyama na binadamu wangeweza kula

kulima

kufanya kila kitu alichopaswa kufanya ili kwamba mimea iweze kuota vizuri

ukungu

Yawezekana maana yake ni 1) kitu kama umande au ukungu wa asubuhi au 2) chemichemi kutoka mikondo chini ya ardhi.

uso wote wa ardhi

dunia nzima

Genesis 2:7

aliumba

"alifinyanga" au "alifanya" au "aliumba"

mtu ... mtu

"binadanu ... mtu" au "mwanadamu" sio lazima wa kiume.

tundu la pua

"pua yake"

pumzi ya uhai

"pumzi inayofanya vitu kuishi". Hapa "uhai" una maana ya uhai wa mwili.

bustani

Hii yaweza kuwa shamba la miti ya matunda au eneo lenye kila aina ya miti.

upande wa mashariki

"mashariki"

Genesis 2:9

mti wa uzima

"mti unaowapa watu uzima"

uzima

Hapa ina maana "uzima wa milele" au maisha yasiyokuwa na mwisho.

mti wa ujuzi wa mema na mabaya

"mti unaowapa watu uwezo wa kuelewa mema na mabaya" au "mti unaowafanya watu wale matunda yake na kuwafanya kuelewa mema na mabaya"

mema na mabaya

Huu ni msemo ambao una maana mbili tofauti kabisa na kila kitu katikati. "kila kitu kujumlisha yote mema na mabaya"

katikati ya bustani

"katikati ya bustani". Yawezekana miti hii miwili haikuwa katikati ya bustani kabisa.

Mto ukatoka nje ya Edeni kuitia maji bustani

Bustani ilikuwa Edeni. Mto uliendelea kutiririka kutoka Edeni. "Mto ukatoka kupitia Edeni na kumwagilia bustani"

Genesis 2:11

Pishoni

Huu ni wakati pekee ambapo mto huu unatajwa katika Biblia.

nchi yote ya Havila

"nchi yote inaitwa Havila". Ilikuwa mahali katika jangwa la Arabia.

ambapo kuna dhahabu

Msemo huu unatoa taarifa kuhusu Havila. Baadhi ya lugha hutafsiri kwa sentensi nyingine tofauti. "Kuna dhahabu Havila"

pia kuna bedola na jiwe shohamu

Neno "kuna" lipo kwenye sentensi kwa kuonyesha msisitizo. "Hapa pia ni mahali ambapo watu waweza kupata bedola na mawe ya shohamu"

bedola

Utomvu huu hutoka katika mti na hutoa harufu nzuri. Bedola hunata na hutoka katika mti fulani na yaweza kuwaka moto.

jiwe shohamu

"mawe ya shohamu". Shohamu ni aina fulani ya mawe ya urembo.

Genesis 2:13

Gihoni

Hii ni sehemu pekee ya mto huu katika Biblia.

unatiririka kupitia nchi yote ya Kushi

Mto haukufunika nchi yote, lakini ulipanda katika sehemu za nchi.

nchi yote ya Kushi

"nchi nzima inayoitwa Kushi"

ambao unatiririka mashariki mwa Ashuru

"ambao unatiririka katika nchi mashariki mwa mji wa Ashuru." Mto wa Hidekeli unatiririka kutoka kaskazini hadi kusini. Msemo "unatiririka mashariki mwa Ashuru" unatoa taarifa kuhusu mahali mto Hidekeli ulipo. Baadhi ya lugha hutafsiri katika sentensi tofauti. "na hutiririka mashariki mwa Ashuru"

Genesis 2:15

bustani ya Edeni

"bustani iliyokuwa Edeni"

kuilima

"kuilima". Hii ina maana ya kufanya kila kitu cha muhimu ili mimea iweze kuota vizuri.

kuitunza

kuilinda dhidi ya mambo mabaya yanayoweza kuikuta

kutoka kwenye kila mti bustanini

"Tunda katika kila mti la bustani"

wewe

kiwakilishi ni cha kipekee

waweza kula kwa uhuru ...usile

Katika baadhi ya lugha ni kawaida kusema kile ambacho hakiruhusiwi na kisha kusema kile ambacho hakiruhusiwi.

waweza kula kwa uhuru

"waweza kula bila kizuizi"

mti wa ujuzi wa mema na mabaya

"mti unaowapa watu uwezo wa kuelewa mema na mabaya" au "mti unaowafanya watu wanaokula matunda yake kujua mambo mazuri na mambo mabaya.

usile

"sitakuruhusu ule" au "haupaswi kula"

Genesis 2:18

Nitamfanyia msaidizi anaye mfaa

"nitafanya msaidizi ambaye ni sahihi kwa ajili yake"

kila mnyama wa kondeni na kila ndege wa angani

Misemo ya "wa kondeni" na "wa angani" inatuambia mahali ambapo wanyama na ndege hupatikana mara kwa mara. "kila aina ya wanyama na ndege"

wanyama wote

"wanyama wote ambao watu huwachunga"

hapakuwa na msaidizi wa kumfaa yeye

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "hapakuwa na msaidizi aliyekuwa sahihi kwa ajili yake"

Genesis 2:21

akaleta usingizi mzito kwa mtu huyu

"alisababisha mwanamume kulala sana." Usingizi mzito ni wakati ambapo mtu kalala na hawezi kubughudhiwa kirahisi au kuamshwa.

Kwa ubavu ... akafanya mwanamke

"Kutoka ubavuni... alimuumba mwanamke." Ubavu ni nyenzo ambayo Mungu alimuumba mwanamke.

kwa sasa, huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu

"Hatimaye, mifupa ya huyu ni kama ya kwangu, na nyama yake ni kama nyama yangu". Baada ya kutazama miongoni mwa wanyama wote kwa ajili ya mwenzi na kukoswa, hatimaye akamwona mtu kama yeye ambaye angeweza kuwa mwenzi wake. Yawezekana mwanamume alionyesha hisia za faraja na furaha.

nyama

Hii inamaanisha sehemu laini za mwili kama ngozi na msuri.

ataitwa 'mwanamke,' kwa sababu ametwaliwa katika mwanaume

"Neno la Kihebrania la 'mwanamke' linafanana na neno la Kihebrania kwa ajili ya 'mwanamume'.

Genesis 2:24

Taarifa ya jumla

Kinachofuata kimeandikwa na mwandishi. Mwanamume hakusema vitu hivi.

Kwa hiyo

"Hii ni kwa sababu"

mwanaume atawaacha baba yake na mama yake

"mwanamume ataacha kuishi kwenye nyumba ya baba na mama yake." Hii inahusu wanamume kwa ujumla. Hailengi mwanamume fulani katika muda fulani.

watakuwa mwili mmoja

Lugha hii inaongelea tendo la ngono kana kwamba miili inakutana pamoja na kuwa kama mwili mmoja. "miili yao miwili itakuwa mwili mmoja"

Wote wawili walikuwa uchi

Neno "walikuwa" linamaana ya mwanamume na mwanamke ambao Mungu aliwaumba.

uchi

"kutovaa mavazi"

lakini hawakuona aibu

"hawakuona aibu kwa kuwa uchi"

Genesis 3

Genesis 3:1

Sasa

Mwandishi anaanza sehemu mpya ya simulizi.

mwerevu kuliko

"mjanja zaidi" au "mwenye akili ya kupata kile atakacho kwa kusema uongo"

Je ni kweli Mungu amesema, 'Msile ... bustanini?

Nyoka anajifanya kushangazwa ya kwamba Mungu alitoa sheria hii. Swali hili la balagha laweza kutafsiriwa kama kauli. "Nashangaa ya kwamba Mungu, "Msile ... bustanini."

Msile

Neno "msile" ni wingi na linamaasha mwanamume na mwanamke

Twaweza kula ... Mungu amesema, 'msile'

Hawa alimwambia nyoka ambacho Mungu aliwaruhusu kufanya kwanza na kisha kile Mungu alichowazuia kufanya. Baadhi ya lugha zingesema kile walichozuiwa kufanya kwanza na kisha kusema kile walichoruhusiwa kufanya.

Twaweza kula

"Tunaruhusiwa kula" au "Tunayo ruhusa ya kula"

Msile ... wala ... mtakufa

Neno "msile" ni wingi na linamaasha mwanamume na mwanamke

Msile

"Hampaswi kula" au "Msile"

msiuguse

"na hampaswi kuigusa" au "na msiuguse"

Genesis 3:4

Wewe ... yenu ... hamtakufa

Maneno haya yanamaanisha mwanamume na mwanamke na kwa hiyo yako katika matumizi mawili au wingi.

macho yenu yatafumbuliwa

"macho yenu yatafumbuliwa." Lugha hii ina maana "utakuwa na utambuzi wa mambo." Maana hii yaweza kutajwa wazi. "Itakuwa kana kwamba macho yenu yamefumbuliwa"

mkijua mema na mabaya

Hapa "mema na mabaya" ni msemo ambao unalenga maana zote mbili kabisa na kila kitu katikati. "kujua kila kitu, ikiwemo mema na mabaya"

na kuwa unapendeza macho

"mti ulipendeza kutazama" au"ulikuwa mzuri kuangalia" au "au ulikuwa mzuri sana"

na kwamba mti ulitamanika kwa kumfanya mtu awe mwerevu

"naye alitaka matunda ya mti kwa sababu ingeweza kumfanya mtu awe mwerevu" au "naye alitaka matunda yake kwa sababu yangemfanya kuelewa kipi kizuri na kibaya kama vile Mungu afanyavyo.

Genesis 3:7

Macho ya wote wawili yalifumbuliwa

"Kisha macho yao yakafumbuliwa" au "Wakapata ufahamu" au "Wakaelewa"

Wakashona

"wakakaza" au"wakaunganisha"

majani ya miti

Iwapo watu hawajui majani ya miti yakoje, hii yaweza kutafsiriwa kama "majani makubwa ya mti" au kwa wepesi "majani makubwa"

na wakatengeneza vya kujifunika kwa ajili wao wenyewe

Walifanya hivi kwa sababu walikuwa na aibu. Taarifa hii inayojitokea yaweza kufanywa dhahiri kama itahitajika. "na wakajivika navyo kwa sababu walikuwa na aibu"

majira ya kupoa kwa jua

"katika kipindi hicho cha siku ambapo hewa tulivu huvuma"

kutoka kwa uwepo wa Yahwe Mungu

"kuepuka uwepo wa Yahwe Mungu" au "ili kwamba Yahwe Mungu asiweze kuwaona" au "kutoka kwa Yahwe Mungu"

Genesis 3:9

uko wapi?

"Kwa nini unajaribu kujificha kwangu?" Mungu alijua mwanamume alikuwa wapi. Mwanamume alipojibu, hakusema yupo wapi bali alisema kwa nini amejificha.

"uko"

Katika mstari wa 9 na 11, Mungu alikuwa akizungumza na mwanamume.

nilikusikia

"Nilisikia sauti uliyokuwa unaifanya"

Ni nani alikwambia

Mungu alijua jibu la swali hili. Aliuliza ili kumlazimisha Adamu akiri kuwa hakumtii Mungu.

Je umekula ... kutoka?

Kwa mara nyingine, Mungu alijua kuwa hiki kimetokea. Tafsiri hili swali katika namna ambayo inaonyesha Mungu anamlaumu Adamu kwa kutokutii kwake. Sentensi yaweza kutafsiriwa kwa kauli hii. "Umekula ..kutoka."

Genesis 3:12

Nini hiki ulichofanya?

Mungu alikwishajua ni nini mwanamke alichofanya. Alipouliza swali hili, alikuwa akimpatia nafasi ajieleze kuhusu lile jambo, na alikuwa akionyesha kusikitishwa kwake kwa kile alichokifanya.Lugha nyingi hutumia maswali ya balagha kwa ajili ya kukemea na kukaripia. "Umefanya jambo baya"

Genesis 3:14

umelaaniwa wewe mwenyewe

"wewe peke yako umelaaniwa." Neno "laana" lipo kwanza kwa Kiebrania ili kuweka msisitizo ya tofauti kati ya baraka ya Mungu kwa wanyama na laana juu ya nyoka. Hii ni laana, au namna ambavyo laana zilitamkwa. Kwa kutamka laana hii, Mungu alifanya itokee.

wanyama wote wa kufugwa na wanyama wote wa mwituni

"wanyama wote wa kufugwa na wanyama wote wa mwitu"

Itakuwa kwa tumbo lako utakwenda

"Utasogea kwenye ardhi kwa kutumiatumbo lako". Maneno "itakuwa kwa tumbo lako" huja kwanza kuweka msisitizo ya tofauti kati ya njia ya wanyama wengine wanavyosogea kwa kutumia miguu yao na njia ya nyoka atakavyotelezateleza kwa tumbo lake. Hii pia ni sehemu ya laana.

mavumbi utakula

"utakula mavumbi". Maneno "ni mavumbi" huja kwanza kuweka msisitizo ya tofauti kati ya mimea juu ya ardhi ambayo wanyama wengine hula na chakula kichafu cha ardhi ambacho nyoka angekula. Hii ni sehemu ya laana.

uadui kati yako na mwanamke

Hii inamaana ya kwamba nyoka na mwanamke wangekuja kuwa maadui.

uzao

"mtoto" au "kizazi". Neno "uzao" linamaanisha nini mwanamume huweka ndani ya nwanamke kusababisha mtoto kukua ndani ya mwanamke. Kama neno la "mtoto" linaweza kumaanisha zaidi ya mtu mmoja, kama neno "vizazi".

Atakujeruhi ... kisigino chake

Maneno "wako" na "wake" yanamaanisha uzao wa mwanamke. Iwapo "uzao" ulitafsiriwa kwa wingi, hii yaweza tafsiriwa kama "watajeruhi .. visigino vyao"; kwa hali hii, "wao" na "yao" hutumika kutafsiri kiwakilishi kimoja.

Atakujeruhi

"ponda" au "kujeruhi" au "shambulia"

Genesis 3:16

nitaongeza uchungu wako sana

"Nitafanya maumivu yako kuongezeka sana" au "Nitafanya maumivu yako kuwa makali sana"

wakati wa kuzaa watoto

"katika kuzaa watoto" au "utakapozaa watoto"

Tamaa yako itakua kwa mume wako

"Utakuwa na tamaa kubwa kwa mume wako." Maana yake yaweza kuwa 1) "Utataka kuwa na mume wako sana" au 2) "Utataka kumuongoza mume wako"

atakutawala

"atakuwa bwana wako" au "atakuongoza"

Genesis 3:17

Adamu

Jina Adamu ni sawa na jina la Kiebrania kwa ajili ya neno "mwanamume". Baadhi ya tafsiri husema "Adamu" na baadhi husema "mwanamume". Unaweza kusema yoyote kati yao maana hulenga mtu mmoja.

umesikiliza sauti ya mke wako

Hii ni lahaja. "umetii kile mkeo kakuambia"

umekula kutoka katika mti

Unaweza kusema ni nini kile walichokula. "wamekula tunda la mti" au "wamekula sehemu ya matunda ya mti"

usile matunda yake

"Hutakiwi kula kutoka kwake" au "Usile matunda yake"

ardhi imelaaniwa

Neno "laana" hujitokeza kwenye sentensi kuweka msisitizo ya kwamba ardhi, ambayo ilikuwa "nzuri" imekuwa chini ya laana ya Mungu sasa. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Ninalaani ardhi"

kupitia kazi yenye maumivu

"kwa kufanya kazi ngumu"

utakula

Neno "utakula" linamaanisha ardhi ambayo ni ufafanuzi wa sehemu ya mimea, ambayo huota ardhini na watu hula. "utakula kile kiotacho kutoka kwake"

mimea ya shambani

Maana yaweza kuwa 1) "mimea unayoitunza shambani mwako" au 2) "mimea ya mwitu inayoota katika mashamba yako"

Kwa jasho la uso wako

"Kwa kufanya kazi ngumu na kufanya uso kutoka jasho"

utakula mkate

Hapa neno "mkate" ni kiwakilishi kwa chakula kwa ujumla. "utakula chakula"

mpaka utakapo irudia ardhi

"hadi utakapokufa na mwili wako unawekwa ndani ya ardhi." Kwa baadhi ya tamaduni, waliweka miili ya watu waliokufa kwenye shimo ardhini. Kazi ya mwanamume haikamiliki hadi kipindi cha kifo na kuzikwa kwake.

kwa kuwa wewe ni mavumbi na kwenye mavumbi utarudi

Nimekufanya kutoka kwenye udongo, kwa hiyo mwili wako utakuwa udongo tena".

Genesis 3:20

Mwanamume

Baadhi ya tafsiri husema "Adamu".

akaita mke wake jina Hawa

"alimpa mke wake jina la Hawa" au "alimuita mkewe Hawa"

Hawa

Neno Hawa linafanana na neno la Kihebrania lenye maana ya "wenye uhai".

wote wenye uhai

Neno hapa "wenye uhai" linamaanisha watu. "watu wote"

mavazi ya ngozi

"mavazi yanayotengenezwa kwa ngozi ya wanyama"

Genesis 3:22

Mwanamume

Maana yaweza kuwa 1) Mungu alimaanisha binadamu mmoja, mwanamume au 2) Mungu alikuwa akimaanisha binadamu kwa ujumla, kwa hiyo ilimaanisha mwanamume na mke wake. Hata kama Mungu alikuwa akizungumza kuhusu mtu mmoja, alichosema kiliwahusu wote wawili.

kama mmoja wetu

"kama sisi". Kiwakilishi "sisi" ni wingi.

ajuaye mema na mabaya

Hapa "mema na mabaya" ni msemo ambao unamaana ya tofauti zote mbili na kila kitu katikati. "kujua kila kitu, ikiwemo mema na mabaya"

hataruhusiwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Sitamruhusu"

mti wa uzima

"mti unaowapa watu uzima"

ardhi ambayo kwahiyo alikuwa ametwaliwa

"ardhi kwa maana alichukuliwa kutoka ardhini". Hii haimaanishi sehemu moja husika katika nchi ambayo Mungu alimchukua.

Kwa hiyo Mungu akamfukuza mtu huyu nje ya bustani

"Mungu alimlazimisha mwanamume aondoke bustanini." Hii inamaanisha tukio la 3:22, ambapo inasema "Yahwe Mungu alimfukuza kwenye bustani ya Edeni". Mungu hakumfukuza mwanamume mara ya pili.

kulima

Hii ina maana kinachohitajika ili mimea iweze kuota vizuri.

ili kulinda njia ya kwenda kwenye mti wa uzima.

"ili kuzuia watu wasiende kwenye mti wa uzima"

upanga wa moto

Maana yaweza kuwa 1) upanga ambao unatoa moto au 2) moto ulikuwa na umbo kama upanga.

Genesis 4

Genesis 4:1

Mwanume

"binadamu" au "Adamu"

akalala na

"akamjua"

nimezaa mwanaume

Neno la "mwanamume" linamuelezea binadamu wa kiume, tofauti na mtoto mchanga au kijana. Kama hiyo italeta kuchanganya, inaweza kutafsiriwa kama "kijana wa kiume" au "mvulana" au "mtoto mchanga wa kiume" au "

Kaini

Watafsiri wanaweza kuweka taarifa fupi ambayo inasema "Jina la Kaini linafanana na neno la Kiebrania linalmaanisha "zaa". Hawa alimuita Kaini kwa sababu alimzaa.

Kisha akazaa

Hatujui ni muda gani ulipita katikati ya kuzaliwa kwa Kaini na Habili. Yawezekana walikuwa mapacha, au Habili alizaliwa baada ya Hawa kupata mimba tena. Kama

alilima

Hii ina maana alifanya kila kitu alichopaswa kufanya ili kwamba mimea iweze kuota vizuri.

Genesis 4:3

Ikawa kwamba

Msemo huu unatumika kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi. Kama lugha yakoin njia ya kufanya hivi, basi tumia njia hii.

baada ya muda

Maana yake yaweza kuwa 1) "baada ya muda kupita" au 2) "kwa muda sahihi"

mazao ya ardhi

Hii inamaanisha chakula kilichotoka kwa mimea aliyoitunza."mazao" au "mavuno"

sehemu zilizonona

Hii inamaanisha sehemu zilizonona za kondoo alizoua, ilikuwa ni sehemu bora zaidi ya mnyama. "baadhi ya sehemu zao zilizonona"

akamkubali

"alipendezwa naye" au "alifurahishwa naye"

alikasirika sana

Baadhi la lugha zina lahaja kwa neno hasira kama "aliwaka" au "hasira yake iliwaka".

ukakunjamana

Hii ina maana muonekano wa uso wake ulionyesha ya kuwa alikuwa amekasirika au ana wivu. Baadhi ya lugha zina lugha ambayo inaelezea sura inavyoonekana anapokuwa na hasira.

Genesis 4:6

kwa nini umekasirika na kwa nini uso wako umekunjamana?

Mungu alitumia maswali haya la balagha kumwambia Kaini ya kwamba hakuwa sahihi kuwa na hasira na kukunjamana sura. Yawezekana yalitumika kumpatia Kaini nafasi ya kutubu makosa yake.

Kama ... je hutapata kibali?

Mungu alitumia swali hili la balagha kumkumbusha Kaini juu ya jambo ambalo Kaini alipaswa kulifahamu. "Unajua ya kwamba ukifanya lilio sahihi, nitakukubali"

lakini kama hutafanya ... inakupasa uishinde

Mungu anazungumzia dhambi kana kwamba ni binadamu. "Lakini kama hutafanya kilicho sahihi, utatamani kufanya dhambi zaidi, na kisha utatenda matendo ya dhambi. Unatakiwa kukataa kuitii"

dhambi iko inakuotea ... kukutawala

Hapa dhambi inazungumziwa kama mnyama mwitu hatari anayesubiri nafasi ya kumshambulia Kaini. "utakuwa na hasira sana utashindwa kuizuia dhambi"

dhambi

Lugha ambazo hazina nomino yenye maana ya "dhambi" zaweza kutafsiri hii kama "tamaa yako kutenda dhambi" au "mambo mabaya unayotaka kufanya".

inakupasa uishinde

Yahwe anazungumzia tamaa ya Kaini kutenda dhambi kana kwamba ni mtu ambaye Kaini anapaswa kumtawala. "unapaswa kuitawala ili usitende dhambi"

Genesis 4:8

Kaini akamwambia Habili ndugu yake

Baadhi ya lugha zinahitaji kuongeza taarifa inayojitokeza ya kwamba Kaini alizungumza na ndugu yake kuhusu kwenda mashambani.

ndugu

Habili alikuwa ndugu yake Kaini. Baadhi ya lugha zinaweza kutumia neno kwa ajili ya "ndugu mdogo"

aliinuka dhidi

"alimshambulia"

Ndugu yako Habili yuko wapi?

Mungu alijua ya kwamba Kaini alimuua Habili, lakini alimuuliza Kaini swali hili ili Kaini aweze kujibu.

Je mimi ni mlinzi wa ndugu yangu?

Kaini alitumia swali hili la balaghaili kukwepa kusema ukweli. Hii yaweza kutafsiriwa katika msemo. "Mimi sio mlinzi wa ndugu yangu!" au "Kumtunza ndugu yangu sio kazi yangu!"

Genesis 4:10

umefanya nini?

Mungu alitumia swali la balagha kumkaripia Kaini. Hii yaweza kutafsiriwa kama msemo. "Ulichofanya ni kibaya"

damu ya ndugu yako inaniita mimi

Damu ya Habili ni lugha kwa ajili ya kifo chake, kana kwamba ni mtu anayemwita Mungu kumuadhibu Kaini. "Damu ya ndugu yako ni kama mtu akiniita kumuadhibu yule aliyemuua"

sasa umelaaniwa wewe kutoka ardhini

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Ninakulaani ili usiweze kuotesha chakula kutoka ardhini"

ambayo imefungua kinywa chake kupokea damu ya ndugu yako

Mungu anazungumzia ardhi kana kwamba ni mtu awezaye kunywa damu ya Habili. "ambayo imelowa kwa damu ya ndugu yako"

kutoka mikononi mwako

Mungu anazungumzia mkono wa Kaini kana kwamba umemwaga damu ya Habili katika "mdomo" wa ardhi. "iliyomwagwa ulipomuua" au "kutoka kwako"

ilima

Hii inamaanisha kufanya kila liwezekanalo ili mimea iweze kuota vizuri.

haita kuzalia wewe nguvu yake

Ardhi inapewa utu kana kwamba ni binadamu anayepoteza nguvu. "ardhi haitakuzalia chakula cha kutosha kwa ajili yako"

mkimbizi na mtu asiye na makao

Unaweza kuunganisha maneno haya pamoja. "mkimbizi asiye na makao"

Genesis 4:13

sitaonekana mbele ya uso wako

Msemo wa "uso wako" unawakilisha uwepo wa Mungu. "Sitaweza kuzungumza na wewe"

mkimbizi na mtu nisiye na makao

mtu asiye na makao

kisasi kitakuwa juu yake mara saba

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Nitachukua kisasi juu yake mara saba" au "Nitamuadhibu mtu yule mara saba kwa ukali kama navyokuadhibu"

asimshambulie

"hatamuua Kaini"

Genesis 4:16

akatoka mbele ya uwepo wa Yahwe

Ingawa Yahwe yupo kila mahali, lahaja hii inamzungumzia Kaini kana kwamba alienda mbali sana. "aliondoka kutoka mahali ambapo Yahwe alizungumza naye"

Nodi

Neno Nodi linamaana ya "mkimbizi"

akamjua

akamjua

Akajenga mji

"Kaini akajenga mji"

Genesis 4:18

Kwa Henoko akazaliwa Iradi

Inasemekana ya kwamba Henoko alikuwa na kuoa mwanamke. "Henoko alikua na kuoa na akawa baba kwa mtoto ambaye alimuita Iradi"

Iradi akamzaa Mehuyaeli

"Iradi alipata mtoto na kumuita Mehuyaeli"

Ada ... Sila

majina ya wanawake

Genesis 4:20

Ada ... Sila

majina ya wanawake

alikuwa baba yao na wale walioishi hemani

Maana yake yaweza kuwa 1) "Alikuwa binadamu wa kwanza kuishi hemani" au 2) "Yeye na uzao wake waliishi hemani"

walioishi hemani ambao wanafuga wanyama

watu wanaoishi hemani na kufuga wanyama

alikuwa baba yao na wale wapigao kinubi na filimbi

Maana yake yaweza kuwa 1) "Alikuwa mtu wa kwanza kupiga kinubi na filimbi" au 2) "Yeye na uzao wake walipiga kinubi na filimbi".

Tubal Kaini, mfua vyombo vya shaba na chuma

"Yubal Kaini. alitengeneza vyombo vya shaba na chuma"

chuma

Hii ni metali yenye nguvu sana iliyotumika kutengeneza vyombo, vifaa na silaha.

Genesis 4:23

Ada .. Sila

majina ya wanawake

sikieni sauti yangu ... sikilizeni nisemacho

lameki alisema jambo moja mara mbili kuonyesha msisitizo. Sauti yake ni lugha nyingine kwa utu wake wote. "nisikilizeni kwa makini"

mtu ... kijana

Lameki alimuua mtu mmoja tu

kwa kunijeruhi ... kwa kunichubua

"kwa sababu alinijeruhi ... kwa sababi alinichubua" au "kwa sababu aliniumiza"

Ikiwa Kaini atalipiwa kisasi mara saba, ndipo Lameki

Lameki anajua ya kwamba Mungu atalipa kisasi kwa ajili ya Kaini mara saba. "Kwa maana Mungu atamuadhibu yeyote atakayemuua Kaini mara saba, Lameki"

ndipo Lameki atalipiwa kisasi mara sabini na saba

mara saba - Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "yeyote atakayeniua, Mungu atamuadhibu mara sabini na saba"

sabini na saba

saba - 77

Genesis 4:25

akamjua

akamjua

na akasema, " Mungu amenipatia mtoto mwingine wa kiume

Hii ni sababu ya yeye kumuita Sethi. Hii inaweza kuwekwa dhahiri. "na ikaeleza, 'Mungu amenipa mtoto mwingine'"

Sethi

Hili jina linaonekana kama neno la Kiyahudi lenye maana ya "amenipatia"

Mtoto wa kiume alizaliwa kwa Seth

Hii inaweza kuwekwa dhahiri. "mke wa Sethi alimzalia mtoto wa kiume"

kuliitia jina la Yahwe

Hii ni mara ya kwanza watu wanamuita Mungu kwa jina la Yahwe. Hii inaweza kuwekwa dhahiri. "kumuabudu Mungu kwa kutumia jina la Yahwe"

Genesis 5

Genesis 5:1

Taarifa ya jumla:

Huu ni mwanzo wa orodha ya uzao wa Adamu.

katika mfano

Msemo huu unamaanisha ya kwamba Mungu aliumba binadamu amfanane yeye. Mstari huu hausemi ni kwa namna gani Mungu aliumba wanadamu wawe kama yeye. Mungu hana mwili, kwa hiyo haimaanishi watu wangekuwa kama Mungu. "kuwa kama sisi"

walipoumbwa

Hii inaweza kufanywa katika hali ya kutenda. "alipowaumba"

Genesis 5:3

130 ... mia nane

Watafsiri wanaweza kuandika tarakimu "130" na "800" au maneno "mia moja na thelathini" na "mia nane".

akamzaa mwana katika sura yake

"akamzaa mwana wa kiume"

katika sura yake mwenyewe, kwa mfano wake

Misemo hii miwili inamaana moja. Inatumika kama kumbukumbu ya kwamba Mungu alimuumba binadamu katika mfano wake.

Sethi

Sethi

Akawazaa wana wengi waume na wake

"Akawa na wana zaidi wa kiume na kike"

kisha akafariki

Msemo huu utarudiwa katika sura yote. "Kisha akaafa"

Adamu akaishi miaka 930

Watu walikuwa wakiishi muda mrefu sana. "Adamu aliishi jumla ya miaka 930"

Genesis 5:6

akawa baba wa Enoshi

Hapa "baba" inamaana ya baba mzazi, na sio babu. "akamzaa mwana wake wa kiume Enoshi"

Enoshi

Hili ni jina la mtu

naye akawa baba wa wana wengi waume na wake

"na akawa na wana zaidi wa kiume na kike"

Sethi akaishi miaka 912

"Sethi aliishi jumla ya miaka 912"

kisha akafariki

"Kisha akafa"

Genesis 5:9

Taarifa ya Jumla:

Kumbukumbu za Mwanzo 5:6-27 zina mfumo mmoja.

Genesis 5:12

Taarifa ya Jumla:

Kumbukumbu za Mwanzo 5:6-27 zina mfumo mmoja.

Genesis 5:15

Taarifa ya Jumla:

Kumbukumbu za Mwanzo 5:6-27 zina mfumo mmoja.

Genesis 5:18

Taarifa ya Jumla:

Kumbukumbu za Mwanzo 5:6-27 zina mfumo mmoja.

Genesis 5:21

akawa baba wa Methusela

"akapata mwana wake wa kiume Methusela"

Methusela

Hili ni jina la mwanamume

Henoko akaenenda na Mungu

Kuenenda na mtu ni sitiari ya kuwa na uhusiano wa karibu na yeye. "Henoko alikuwa na uhusiano wa karibu na Mungu" au "Henoko aliishi kwa umoja na Mungu"

Akawa baba wa wana zaidi wa kiume na kike

"Akawa na wana zaidi wa kiume na kike"

Henoko aliishi miaka 365

"Henoko aliishi jumla ya miaka 365"

kisha alitoweka

Neno "alitoweka" linamaanisha Henoko. Hakuwa duniani tena.

kwa kuwa Mungu alimtwaa

Hii inamaana Mungu alimtwaa Henoko awe naye.

Genesis 5:25

Taarifa ya Jumla:

Kumbukumbu za Mwanzo 5:6-27 zina mfumo mmoja.

Lameki

Lameki huyu ni tofauti na Lameki wa 4:18

Genesis 5:28

akawa baba wa mwana wa kiume

"akapata mwana wa kiume"

Nuhu

Jina hili linafanana na jina la Kiyahudi lenye maana ya "pumziko".

katika kazi yetu na kutoka katika kazi ya taabu ya mikono yetu

Lameki anasema jambo hilo hilo mara mbili kusisitiza jinsi kazi ilivyo ngumu. "kwa kufanya kazi sana kwa mikono yetu"

Genesis 5:30

Lameki aliishi miaka 595

"Lameki aliishi jumla ya miaka ya 777"

Genesis 5:32

akawa baba wa

"akazaa watoto wake wa kiume". Hii haituambii kama wana wa kiume walizaliwa katika siku moja au mika tofauti.

Shemu, Hamu, na Yafethi

Yawezekana wana hawa wa kiume hawajaorodheshwa kufuata kuzaliwa kwao. Kuna mjadala kuhusu nani alikuwa mkubwa. Epuka kutafsiri haya majina na kuonyesha ya kwamba orodha ipo katika mpangilio wa umri wao.

Genesis 6

Genesis 6:1

Ikawa wakati

Msemo huu unatumika hapa kuonyesha alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

wana wa kike wakazaliwa kwao

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "wanawake wakazaa mabinti"

wana wa Mungu

Haipo wazi kama hii inamaanisha viumbe wa mbinguni au wanadamu. Kwa vyovyote vile, walikuwa viumbe ambao Mungu aliumba. Baadhi wanaamini maneno haya yanamaanisha malaika waliomuasi Mungu, yaani, roho chafu au mapepo. Wengine wanadhani hii inamaanisha watawala wa kisiasa wenye nguvu, na wengine wanadhani hii inamaanisha uzao wa Sethi.

roho yangu

Hapa Yahwe anaongelea kuhusu yeye mwenyewe na roho wake, ambaye ni Roho wa Mungu.

nyama

Hii ina maana wana mwili ambayo itakufa siku moja

Wataishi miaka 120

Maana yaweza kuwa 1) urefu wa kawaida wa watu ingepungua hadi miaka 120. "Hawataishi zaidi ya miaka 120" au 2) katika miaka 120 kila mtu atakufa. "Wataishi miaka 120 tu"

Genesis 6:4

Majitu makubwa

warefu sana, watu wakubwa

Hii ilitokea wakati

"Hawa majitu makubwa walizaliwa kwa sababu"

wana wa Mungu

Haipo wazi kama hii inamaanisha viumbe wa mbinguni au wanadamu. Kwa vyovyote vile, walikuwa viumbe ambao Mungu aliumba. Baadhi wanaamini maneno haya yanamaanisha malaika waliomuasi Mungu, yaani, roho chafu au mapepo. Wengine wanadhani hii inamaanisha watawala wa kisiasa wenye nguvu, na wengine wanadhani hii inamaanisha uzao wa Sethi.

Hawa walikuwa watu hodari zamani

"Majitu makubwa walikuwa wanaume hodari walioishi zamani" au "Hawa watoto wakakua kuja kuwa wapiganaji hodari walioishi zamani"

watu hodari

wanaume ambao ni wajasiri na washindi katika vita

watu wenye sifa

"watu maarufu"

Genesis 6:5

mwinamo

"mwelekeo" au "tabia"

mawazo ya mioyo yao

Mwandishi anazungumzia juu ya moyo kana kwamba ni sehemu ya mwili unaofikiri. "mawazo yao ya ndani ya siri"

ikamuhuzunisha moyo wake

Mwandishi anazungumzia juu ya moyo kana kwamba ni sehemu ya mwili unaoweza kuhisi huzuni. "alikuwa na huzuni sana mno juu ya hili"

Genesis 6:7

Nitamfutilia mbali mwanadamu ... katika uso wa nchi

Mwandishi anamzungumzia Mungu kuua watu kana kwamba Mungu alikuwa akisafisha uchafu katika nchi tambarare. "Nitawaangamiza wanadamu ..ili kwamba kusiwepo na watu katika nchi"

Nitamfutilia mbali mwanadamu ambaye nimemuumba

Baadhi ya lugha hutafsiri hii kama sentensi mbili. "Niliumba mwanadamu. Nitamfutilia mbali"

Nitamfutilia

"kuangamiza kabisa". Hapa "kuangamiza" inatumika katika hali ya hasi, kwa maana Mungu anazungumzia juu ya kuangamiza watu kwa sababu ya dhambi yake.

Nuhu akapata neema ya upendeleo machoni pa Yahwe

"Yahwe alimtazama Nuhu kwa upendeleo" au "Yahwe alifurahishwa na Nuhu"

machoni pa Yahwe

Hapa "machoni" inamaana ya mtazamo au mawazo. "katika mtazamo wa Yahwe" au " katika mawazo ya Yahwe"

Genesis 6:9

Taarifa ya Jumla:

Hii inaanza simulizi ya Nuhu, ambayo inayoendelea mpaka kwenye sura ya 9.

Haya yalikuwa matukio yanayomhusu Nuhu

"Hii ni taarifa ya Nuhu"

alitembea na Mungu

Kutembea na mtu ni sitiari ya kuwa na uhusiano wa karibu na yeye. "Nuhu alikuwa na uhusiano wa karibu na Mungu" au "Nuhu aliishi kwa umoja na Mungu"

Nuhu akafanyika baba wa wana watatu wa kiume

"Nuhu akawa na wana watatu wa kiume" au "Mke wa Nuhu akawa na wana watatu wa kiume"

Shemu, Hamu, na Yafethi.

"Wana wa kiume hawajaorodheshwa katika mpangilio wa kuzaliwa"

Genesis 6:11

Nchi

Maana yaweza kuwa 1) watu walioishi duniani au 2) "Dunia yenyewe"

iliharibika

Watu waliokuwa wakifanya uovu inazungumziwa kana kwamba walikuwa chakula kilichooza. "ilioza" au "ilikua na ouvu sana"

mbele za Mungu

Maana yaweza kuwa 1) "machoni pa Mungu" au 2) "katika uwepo wa Yahwe" kama 4:16.

na ilijaa ghasia

Mwandishi anazungumzia ghasia kana kwamba ni kitu kinachoweza kuwekwa ndani ya chombo na nchi kama chombo. "na kulikuwa na wanadamu wenye vurugu sana nchini" au "kwa sababu ilikuwa imejaa watu waliofanya mambo maovu baina yao"

tazama

Neno "tazama" hapa linatutahadharisha kuwa msikivu kwa taarifa ya kushtukiza inayofuata.

wote wenye mwili

Maana yaweza kuwa 1) wanadamu wote au 2) viumbe vyote vyenye mwili, ikijumlisha wanadamu na wanyama.

wameharibu njia zao

Namna mtu anavyoishi inazungumzwa kana kwamba ilikuwa njia au barabara. "waliacha kuishi kwa njia ambayo Mungu alitaka" au "waliishi katika njia ya uovu"

Genesis 6:13

wenye mwili

Maana yaweza kuwa 1) wanadamu wote au 2) viumbe vyote vyenye mwili, ikijumlisha wanadamu na wanyama.

inchi imejaa ghasia kutokana na wao

"watu nchini kote wana vurugu"

nitawaangamiza wao pamoja na nchi

"Nitawaangamiza wao pamoja na nchi" au "Nitawaangamiza wao nitakapoiangamiza nchi"

safina

Hii inamaanisha sanduku kubwa sana ambalo lingeweza kuelea juu ya maji hata katika dhoruba mbaya. "mtumbwi mkubwa" au "meli" au "tishali"

mti wa mvinje

Watu hawajui haswa huu ulikuwa mti wa aina gani. "mbao iliyotumika kuunda mitumbwi" au "mbao nzuri"

vifunike kwa lami

"sambaza lami juu yake" au "paka lami juu yake". Sababu ya kufanya hivi yaweza kuwekwa wazi: "kufanya isipitishe maji"

lami

Hiki ni kimiminiko chenye mafuta, kizito, na kinatacho ambacho watu huweka nje ya mtumbwi kuzuia maji kupenya katika nafasi za mbao hadi kwenye mtumbwi.

dhiraa

Dhiraa ilikuwa ni namba ya kipimo, kiasi kidogo tu kwa mita moja.

dhiraa mia tatu

"mita 138". Dhiraa mia tatu ni sawa na mita 138"

dhiraa hamsini

"mita ishirini na tatu"

dhiraa thelathini

"mita kumi na nne"

Genesis 6:16

paa la safina

Inawezekana hii lilikuwa paa lililochongeka au lililolala. Kusudi lake lilikuwa kulinda kila kitu ndani ya safina dhidi ya mvua.

dhiraa

Dhiraa ilikuwa ni namba ya kipimo, kiasi kidogo tu kwa mita moja.

ya chini, ya pili na ya tatu

"dari ya chini, ya katikati, na ya juu" au "dari tatu ndani"

dari

"sakafu" au "daraja"

Sikiliza

Mungu alinena hivi ili kusudi kusisitiza ya kuwa angefanya kile alichotarajia kukifanya. "Sikiliza" au "Sikiliza kile nachosema"

nimekaribia kuleta gharika ya maji

"Nimekaribia kutuma mafuriko ya maji" au "ninakaribia kusababisha mafuriko"

mwili wote

Hapa "mwili" inawakilisha viumbe vyote vya mwili, kujumlisha binadamu na wanyama.

wenye mwili wote wakaao ndani ya nchi wenye pumzi ya uhai

Hapa "pumzi" inawakilisha uhai. "inayoishi"

Genesis 6:18

nitalifanya thabiti agano langu na wewe

"fanya agano kati yako na mimi"

na wewe

pamoja na Nuhu

Utaingia ndani ya safina

"Utaingia ndani ya safina" Baadhi ya tafsiri husema "Utaingia ndani mwa safina".

Kwa kila kiumbe hai chenye mwili, viwili vya kila aina utavileta ndani ya safina

"Unapaswa kuleta aina mbili ya kila aina ya kiumbe ndani ya safina"

kiumbe

mnyama ambaye Mungu aliumba

chenye mwili

Maana yaweza kuwa 1) wanadamu wote au 2) viumbe vyote vyenye mwili, ikijumlisha wanadamu na wanyama.

Genesis 6:20

kwa jinsi yake

"wa kila aina tofauti"

kitambaacho ardhini

Hii inamaana ya wanyama wadogo ambao hutambaa juu ya ardhi

viwili vya kila aina

Hii inamaana ya ain mbili ya kila aina ya ndege na mnyama.

viwe salama

"ili uweze kuwaweka wawe hai"

kwako ... kwa ajili yako .. chako

Hii inamaana ya Nuhu na ni katika umoja

chakula kinacholiwa

"chakula ambacho watu na wanyama hula"

Kwa hiyo Nuhu akafanya hivi. kulingana na yote ambayo Mungu alimuagiza, ndivyo alifanya

Sentensi hizi mbili zinamaanisha jambo moja. Sentensi ya pili inafafanua ya kwanza na kuweka msisitizo ya kwamba Nuhu alimtii Mungu. Sentensi hizi zilizo sambamba zinaweza kuunganishwa kuwa kitu kimoja. "Kwa hiyo Nuhu alifanya kila kitu alichoambiwa na Mungu kufanya"

Genesis 7

Genesis 7:1

Taarifa ya jumla:

Matukio ya sura hii yanatokea baadaya Nuhu kujenga safina, kukusanya chakula, na kukiweka ndani ya safina.

Njoo ...katika safina ...utakuja nao

"Ingia ... ndani ya safina .. chukua". Tafsiri nyingi husema "Nenda .. ndani ya safina .. chukua"

wewe

Neno hapa "wewe" linamaana ya Nuhu la lipo katika umoja.

nyumba yako

"familia yako"

mwenye haki mbele yangu

Hii inamaana ya kwamba Mungu alimwona Nuhu kuwa mwenye haki.

katika kizazi hiki

Hii inamaana ya watu wote ambao walikuwa wakiishi katika muda huo. "Kati ya watu wote wanaoishi sasa"

mnyama aliye safi

Huyu alikuwa ni myama ambaye Mungu aliruhusu watu wake wamle na kutoa sadaka.

wanyama wasio safi

Hawa ni wanyama ambao Mungu hakuruhusu watu wale au kutoa sadaka.

kuhifadhi kizazi chao

"ili kwamba waweze kuwa na kizazi kitakachoishi" au "ili kwamba, baada ya gharika, wanyama waendelee kuishi"

Genesis 7:4

siku arobaini mchana na usiku

Hii ilikuwa siku arobaini kamili. Haikuwa jumla ua siku themanini. "siku arobaini mchana na usiku"

hai

Hii inamaana ya uhai wa mwili

Genesis 7:6

Taarifa ya jumla

Mistari ya 6-12 inarudia kwa mara ya pili na kutoa kwa utondoti jinsi gani Nuhu alivyoinbgia ndani ya safina na familia yake pamoja na wanyama katika 7:1. Hili sio tukio jipya.

ilipokuja juu ya nchi

"ilipotokea" au "ikaja juu ya nchi"

kwa sababu ya maji ya gharika

"kwa sababu ya gharika itakayokuja" au "kutoroka maji ya gharika"

Genesis 7:8

Taarifa ya jumla:

Mistari ya 6-12 inarudia kwa mara ya pili na kutoa kwa utondoti jinsi gani Nuhu alivyoinbgia ndani ya safina na familia yake pamoja na wanyama katika 7:1. Hili sio tukio jipya.

Wanyama ambao ni safi

Hawa walikuwa wanyama ambao Mungu aliruhusu watu wake kuwala na kuwatoa kama sadaka kwake.

wanyama ambao si safi

Hawa walikuwa wanyama ambao Mungu hakuruhusu watu wake wale au kuwato kama sadaka kwake.

wawili wawili

Wanyama waliingia kwenye safina katika makundi ya dume mmoja na jike mmoja.

Ikawa kwamba

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama kuhusu tukio muhimu katika simulizi hii. Mwanzo wa gharika.

baada ya zile siku saba

"baadaya siku saba" au"siku saba baadaye"

maji ya gharika yakaja juu ya nchi

Habari inayojitokeza, "ikaanza kunyesha" inaweza kufanywa kuwa wazi. "ikaanza kunyesha na maji ya gharika yakaja juu ya nchi"

Genesis 7:11

Taarifa ya jumla:

Mistari ya 6-12 inarudia kwa mara ya pili na kutoa kwa utondoti jinsi gani Nuhu alivyoinbgia ndani ya safina na familia yake pamoja na wanyama katika 7:1. Hili sio tukio jipya.

Katika mwaka wa mia sita wa maisha yake Nuhu

"Nuhu alipokuwa na umri wa miaka 600"

mwezi wa pili, katika siku ya kumi na saba ya mwezi

Kwa kuwa Musa aliandika kitabu hiki, inawezekana inamaanisha mwezi wa pili katika kalenda ya Kiebrania. Lakini hii haina uhakika

katika siku iyo hiyo

Hii ina maana siku bayana ambapo mvua ilianza. Msemo huu unasisitiza jinsi gani matukio yote makubwa yalivyotokea haraka muda ulipowadia.

chemchemi zote za vilindi vikuu zilipasuka na kufunguka

"maji kutoka chini ya ardhi yalifunguka juu kwenye sakafu ya nchi"

vilindi vikuu

Hii ina maana ya bahari ambalo inasadikiwa lilikuwa chini ya ardhi.

madirisha ya mbinguni yakafunguka

Hii ina maana ya mvua. Inaelezea anga kama dari ambalo hutunza maji juu yake kutodondoka ardhini. Madirisha, au milango, ya anga yalipofunguliwa, maji yalifunguka chini kupitia kwao. "anga ikafungua" au "milango ya anga ikafunguka"

mvua

Mvua kubwa

Genesis 7:13

Taarifa ya jumla

Mistari ya 13-18 inarudia kwa mara ya tatu na kutoa kwa undani kuhusu jinsi gani Nuhu aliingia katika safina pamoja na familia yake na wanyama katika 7:1. Hili si tukio jipya.

Katika siku iyo hiyo

"Katika siku hiyo hasa". Hii ina maana ya siku ambayo mvua ilianza kunyesha. Mistari ya 13-16 inaeleza Nuhu alichofanya kabla tu ya mvua kuanza.

mnyama wa mwitu ... mnyama wa kufugwa ... kila kitambaacho ... ndege

Vikundi hivi vinne vinaorodheshwa kuonyesha ya kwamba kila aina ya mnyama alijumuishwa.

kila kitambaacho

Hii ina maana ya wanyama watambaao juu ya ardhi, kama wanyama wagugunaji, wadudu, mjusi na nyoka.

kwa jinsi yake

"ili kwamba kila aina ya mnyama azalishe zaidi ya kila aina yake"

Genesis 7:15

Taarifa ya Jumla:

Mistari ya 13-18 inarudia kwa mara ya tatu na kutoa ufafanuzi zaidi jinsi gani Nuhu aliingia katika safina pamoja na familia yake na wanyama. Hili sio tukio.

Viwili viwili katika kila chenye mwili

Hapa "mwili" inawakilisha wanyama.

ambacho kilikuwa na pumzi ya uhai

Hapa "pumzi" inawakilisha uhai. "alivyoishi"

kilikuja kwa Nuhu

Neno "kilikuja" linaweza kutafsiriwa kama "alikwenda".

wote wenye mwili

Hapa "mwili" inawakilisha wanyama. "katika kila aina ya mnyama"

akawafungia

Maana kamili yaweza kutajwa wazi. "walipoingia ndani ya safina"

Genesis 7:17

Taarifa ya Jumla:

Mistari ya 13-18 inarudia kwa mara ya tatu na kutoa ufafanuzi zaidi jinsi gani Nuhu aliingia katika safina pamoja na familia yake na wanyama. Hili sio tukio.

na maji yakaongezeka

Hii ilitokea katika kipindi cha siku arobaini wakati maji yalipokuwa yakija. "na maji yakawa na kina kirefu sana"

na kuinua safina

"na ikasababisha safina kuelea"

kuinua juu ya nchi

inasababisha safina kuinuka juu ya nchi" au "safina ilielea juu ya maji ya kina kirefu"

Genesis 7:19

Maji yakaongezeka zaidi juu ya nchi

"Maji yalishinda kabisa nchi"

dhiraa kumi na tano

"mita sita"

Genesis 7:21

vilitembea juu

"vilisogea kote kote" au "vilitangatanga"

viumbe hai vyote kwa wingi vilivyoishi juu ya nchi

Hii ina maanisha wanyama wote wanatembea kote kote juu ya nchi kwa makundi makubwa.

vilivyo pumua pumzi ya uhai kwa njia ya pua

Hapa "pua" inawakilisha mnyama mzima au mwanadamu. "kila mtu apumuaye"

pumzi ya uhai

Maneno "pumzi"na "uhai" yanawakilisha nguvu inayosababisha watu na wanadamu kuwa na uhai.

vilikufa

Hii ina maana kifo cha kimwili

Genesis 7:23

Hivyo kila kilichokuwa hai ... kilifutwa

Ikiwezekana, hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Kwa hiyo kila kiumbe hai ... kikatoweka" au "Kwa hiyo gharika iliangamiza kabisa kila kiumbe hai"

Vyote viliangamizwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mungu aliwaangamiza wote"

kutoka kwenye nchi

"kwa hiyo hawakuwa katika nchi"

na wale waliokuwa naye

"na watu pamoja na wanyama waliokuwa naye"

walisalia

"walibaki" au "waliishi" au"walibaki hai"

Maji yalitawala nchi

"Maji yenye kina kirefu yalifunika nchi yote" au "Maji yalibaki na gharika kubwa juu ya nchi"

Genesis 8

Genesis 8:1

akamtazama

"akamkumbuka" au "alimfikiria"

safina

Hii inamaanisha sanduku kubwa sana ambalo lingeweza kuelea juu ya maji hata katika dhoruba mbaya. "mtumbwi mkubwa" au "meli" au "tishali"

Chemichemi za vilindi pamoja na madirisha ya mbingu vikafungwa

"Maji yaliacha kutoka chini ya ardhi na mvua zikaacha kunyesha." Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mungu alifunga chemichemi za vilindi na madirisha ya mbinguni"

chemichemi za vilindi

"maji kutoka chini ya ardhi"

madirisha ya mbingu vikafungwa

Hii ina maana ya mvua kuacha kunyesha. Hii ina maana ya mvua. Inaelezea anga kama dari ambalo hutunza maji juu yake kutodondoka ardhini. Madirisha, au milango, ya anga yalipofunguliwa, maji yalifunguka chini kupitia kwao. "anga ikafungua" au "milango ya anga ikafunguka"

Genesis 8:4

ikatulia

"ikatua" au "ikasimama juu ya ardhi ngumu"

katika mwezi wa saba, siku ya kumi na saba ya ... mwezi wa kumi

Kwa sababu Musa aliandika kitabu hiki, inawezekana ana maana ya mwezi wa saba na mwezi wa kumu kwa kalenda ya Kihebrania, lakini hii haipo wazi.

Katika siku ya kwanza ya mwezi

"Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kumi"

vikaonekana

Hii inaweza kuwekwa wazi: "ikaonekana juu ya uso wa maji"

Genesis 8:6

Ikatokea kwamba

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi. "Ikawa kwamba"

Ikatokea kwamba ... dirisha la safina ambayo aliitengeneza

Msemo "ambayo alitengeneza" unazungumzia kuhusu madirisha. Baadhi ya lugha zaweza kufanya msemo huu kuwa sentensi tofauti. "Nuhu alitengeneza dirisha katika safina. Ikaja kuwa baada ya siku arobaini ndipo dirisha likafunguliwa"

kunguru

ndege mweusi anayekula zaidi nyama ya mizoga ya wanyama

akaruka mbele na nyuma

Hii ina maana ya kwamba kunguru aliendelea kuacha safina na kurejea.

hadi maji yalipo kauka

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "hadi pale upepo ulipokausha maji" au "hadi maji yalipokauka"

Genesis 8:8

kutua unyayo wake

"kutua" au "kutulia juu ya". Ina maana ya kutua juu ya kitu ili kupumzika kupaa.

unyayo wake ... akarudi ... akamchukua

Neno "njiwa" kwa lugha ya mwandishi ni la kike. Unaweza kutafsiri msemo huu na kiwakilishi cha "hiki ... huyu ... hii" au "yake ... yeye ... yeye" kulingana na namna gani lugha inamfafanua njiwa.

Akanyoosha ... naye

Ukitumia kiwakilishi cha kiume kwa neno "njiwa" inaweza kuhitaji kuongeza jina la Nuhu ili kukwepa mchanganyo. "Nuhu alimtuma njiwa," "Nuhu alinyosha mkono wake mbele" n.k.

Genesis 8:10

Tazama

"Sikiliza kwa makini" au "Hii ni muhimu"

jani bichi la mzeituni lililochumwa

"jani ambalo njiwa alichuma kutoka katika mzeituni"

lililochumwa

"kunyofoa"

Akasubiri siku saba zingine

"Alisubiri tena siku saba"

Njiwa hakurudi kwake tena

Iwapo watu hawataelewa unaweza kutoa sababu wazi: "Hakurudi tena kwake kwa sababu alipata sehemu ya kutua".

Genesis 8:13

Ikawa kwamba

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

katika mwaka wa mia sita na mwaka wa kwanza

"Nuhu alipokuwa na umri wa miaka 601"

mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi

Kwa sababu Musa aliandika kitabu hiki, inawezekana ana maana ya mwezi wa saba na mwezi wa kumu kwa kalenda ya Kiebrania, lakini hii haipo wazi.

maji yalikuwa yamekauka katika nchi

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "maji yaliyofunika nchi yalikauka" au "upepo ulikausha maji yaliyofunika nchi"

kifuniko cha safina

Hii ina maana ya kifuniko kilichozuia maji ya mvua kuingia ndani ya safina.

tazama

Neno "tazama" linatuambia kuwa makini kwa ajili ya taarifa muhimu inayafuatia.

Katika mwezi wa pili, siku ya ishirini na saba ya mwezi

siku ya saba ya mwezi - "Katika siku ya ishirini na saba ya mwezi wa pili." Hii inaweza kuwa na maana ya mwezi wa pili katika kalenda ya Kihebrania, lakini haipo wazi.

nchi ilikuwa imekauka

"ardhi ilikuwa imekauka kabisa"

Genesis 8:15

Toka nje ... 17Wachukuwe

"Ondoka ...Chukua" Baadhi ya tafsiri husoma "Njoo nje ... Leta nje".

kila kiumbe hai chenye mwili

"kila aina ya kiumbe hai" Maana yaweza kuwa 1) wanadamu wote au 2) viumbe vyote vyenye mwili, ikijumlisha wanadamu na wanyama.

kwa kuzaliana na kuongezeka

Hii ni lahaja. Jazeni nchi na watu. Mungu alitaka wanadamu na wanyama kuzaliana, ili waweze kuwa wengi wa aina yao.

Genesis 8:18

Nuhu akatoka nje

Baadhi ya tafsiri husoma "Nuhu akaja nje"

kwa kabila zao

"katika makundi ya aina yao wenyewe"

Genesis 8:20

akajenga madhabahu kwa Yahwe

"akajenga madhabahu kwa makusudi ya Yahwe" au "akajenga madhabahu kwa ajili ya kumuabudu Yahwe." Inawezekana alijenga kwa mawe.

wanyama walio safi ... ndege walio safi

Hapa "safi" ina maana ya kwamba Mungu aliruhusu wanyama hawa kutumika kama sadaka. Baadha ya wanyama hawakutumika kwa ajili ya sadaka na waliitwa "wasio safi".

kutoa sadaka ya kuteketezwa

Nuhu aliwaua wanyama na kuwachoma kabisa kama sadaka kwa Mungu. "aliwachoma wanyama kama sadaka kwa Yahwe"

harufu nzuri ya kuridhisha

Hii ina maana ya harufu nzuri ya nyama ya kuchomwa.

akasema moyoni mwake

Hapa neno la "moyo" lina maana ya mawazo na hisia za Mungu.

laani ardhi

"kuleta madhara makubwa kwenye nchi"

kwa sababu ya mwanadamu

Hii inaweza kuwa wazi: "kwa sababu mwanadamu ni mwenye dhambi"

nia za mioyo yao ni mbaya tokea utoto

"kutoka miaka yao ya utotoni wanakuwa wakifanya mambo maovu" au "walipokuwa wadogo, walitaka kufanya mambo maovu"

nia za mioyo yao

Hapa neno "mioyo" lina maana ya mawazo, hisia, haja na ridhaa ya watu. "mwelekeo wao" au "tabia yao"

tokea utoto

Hii ina maana ya mtoto mwenye umri mkubwa. "kutoka ujana wao"

Wakati nchi isaliapo

"wakati nchi inapoendelea kudumu" au "Kadri nchi inavyoendelea kuwepo"

majira ya kupanda mbegu

"msimu wa kupanda"

baridi na joto, kiangazi na majira ya baridi

Misemo hii miwili ina maana ya aina mbili za majira katika mwaka.

kiangazi

kipindi kikavu na cha joto cha mwaka

majira ya baridi

kipindi cha baridi kidogo na theluji katika mwaka

havitakoma

"havitaacha kuwepo" au "havitaacha kutendeka" . Hii inaweza kuelezwa katika hali ya chanya. "vitaendelea"

Genesis 9

Genesis 9:1

Zaeni, mkaongezeke, na muijaze nchi

Hii ni baraka ya Mungu. Alimwambia Nuhu pamoja na familia yake kuzaliana wanadamu wengine kama wao, ili kwamba wawe wengi wa aina yao. Neno "mkaongezeke" linafafanua jinsi gani wanapaswa "kuzaana"

Hofu na utisho wenu vitakuwa juu ya kila mnyama aliye hai ... na juu ya samaki wote wa baharini

Mwandishi anazungumzia hofu na utisho kana kwamba ni vitu vya mwili ambavyo vingeweza kuwa juu ya wanyama. "Kila mnyama hai ... na samaki wote wa baharini watakua na hofu kubwa sana juu yako"

Hofu na utisho wenu

maneno "hofu" na "utisho" zina maana moja na husisitiza jinsi wanyama walivyokuwa wanaogopa binadamu. "Hofu ya utisho kwako" au "Hofu ya kutisha kwako"

kila mnyama aliye hai juu ya nchi

Hili ni moja kati ya makundi manne ya wanyama ambayo mwandishi ameorodhesha, na sio ufupisho wa wanyama waliosalia atakaowataja hapo baadae

ndege

Huu ni msemo wa jumla kwa vitu vinavyopaa. "wanyama warukao" au "vitu vinavyoruka"

juu ya kila kitu kiendacho chini juu ya ardhi

Hii inajumuisha aina yote ya wanyama.

Vimetolewa katika mikono yenu

Mkono ni lugha mbadala kwa mamlaka ambayo mkono ulikuwa nayo. Hii inaweza kuwa katika hali ya kutenda. "Vimetolewa katika mamlaka yako" au "Nimeviweka chini ya mamlaka yako"

Genesis 9:3

Taarifa ya Jumla:

Mungu anaendelea kuzungumza na Nuhu pamoja na watoto wake.

uhai ... damu

"Damu ni alama ya uhai". "Mungu alikuwa akiwaamuru watu wasile nyama ambayo bado ina damu ndani yake. Walipaswa kutoa kwanza damu"

Genesis 9:5

Taarifa ya Jumla:

Mungu anaendelea kuzungumza na Nuhu pamoja na watoto wake.

Lakini kwa ajili ya damu yenu

Hii inatofautisha damu ya mwanadamu na damu ya wanyama

kwa ajili ya damu yenu

Inaonyesha ya kwamba damu imemwagwa, au imemwagika, au mwagikia. "iwapo yeyote atasababisha damu yako kumwagika" au "iwapo yeyote atamwaga damu yako" au "iwapo yeyote atakuua"

uhai

Hii ina maana ya uhai wa mwili.

nitataka malipo

Malipo haya yana maana kifo kwa yule muuaji, sio fedha. "Nitataka yeyote atakayekuua kulipa"

Kutoka katika mkono

Hapa neno "mkono" lina maana ya yule mtu anayehusika na jambo kutendeka.

Kutoka katika mkono wa kila mnyama nitaitaka

"Nitataka mnyama yeyote atakayetoa uhai wako kulipa"

Kutoka katika mkono wa kila mtu, yaani, kutoka katika mkono wa yule ambaye amemuua ndugu yake, nitataka fidia kwa ajili ya uhai wa mtu huyo.

"Nitataka mtut yeyote atakayetoa uhai wa mtu mwingine kulipa"

Kutoka katika mkono

Msemo huu una maana ya mtu katika hali ya ukaribu sana. "Kutoka kwa mtu huyo kabisa"

ndugu

Hapa "ndugu" inatumika kama kumbukumbu ya jumla kwa jamaa, kama wanajumuiya wa kabila moja, ukoo au kikundi cha watu.

Yeyote amwagaye damu ya mtu, kwa njia ya mtu damu yake itamwagwa

Kumwaga kwa damu ni sitiari kwa ajili ya kuua mtu. Hii ina maanisha kama mtu atamuua mtu, mtu mwingine anapaswa kumuua muuaji. japokuwa, "damu" ina umuhimu sana katika kipengele hichi na inapaswa kutumiwa katika tafsiri ikiwezekana.

kwa sababu ilikuwa ni katika mfano wa Mungu kwamba Mungu alimuumba mtu

"kwa sababu Mungu aliumba watu wafanane na yeye" au "kwa sababu niliumba watu katika mfano wangu"

zaeni na kuongezeka

Hii ni baraka ya Mungu. Alimwambia Nuhu na familia yake kuzaa wanadamu wengine kama wao wenyewe, ili kusudi waweze kuwa wengi zaidi. Neno "kuongezeka" linafafanua jinsi ya wao "kuzaa"

Genesis 9:8

Kisha Mungu akazungumza na Nuhu na wanae pamoja naye

Mungu alikuwa akizungumza nao tayari. Msemo huu unaweka alama ya mabadiliko juu ya kile Mungu alichokuwa akienda kukizungumzia. "Mungu aliendelea kuzungumza na Nuhu pamoja na watoto wake" au "Kisha Mungu akaendelea kusema"

Kwa ajili yangu

Msemo huu unatumika kwa Kiingereza kuweka alama ya mabadiliko juu ya kile Mungu alichokuwa akizungumzia juu ya Nuhu na wanawe walichopaswa kufanya na kuzungumzia juu ya nini Mungu angefanya.

kulithibitisha agano langu pamoja nawe

"fanya agano kati yako na mimi"

Genesis 9:11

Maelezo ya Jumla:

Mungu anaendelea kuzungumza na Nuhu na wanawe.

ninalithibitisha agano langu pamoja nanyi

"kwa kusema hivi, ninafanya agano langu pamoja na wewe"

mwili

Maana zaweza kuwa 1) binadamu wote au 2) wenye viumbe wote, kujumlisha binadamu na wanyama.

Tena hapatatokea gharika ya kuangamiza nchi

"Hakutakuwa tena na gharika ambalo litaangamiza nchi". Kutakuwa na gharika, lakini hazitaangamiza dunia nzima.

ishara

Hii ina maana ya ukumbusho wa jambo lililoahidiwa.

agano ... kwa vizazi vyote vya baadaye

Agano hili linamhusu Nuhu na familia yake na pia vizazi vyote vitakavyofuata.

Genesis 9:14

Maelezo ya Jumla:

Mungu anaendelea kuzungumza na Nuhu na wanawe.

itakuwa nitakapoleta

"Itakapokuwa". Ni jambo ambalo hutokea mara nyingi.

upinde wa mvua ukaonekana

Haipo wazi ni nani atauona upinde wa mvua, lakini kwa sababu agano upo kati ya Yahwe na watu, iwapo utataka kusema nani atauona upinde wa mvua, ni vyema kuwataja wote Yahwe na watu. Hii inaweza kutafsiriwa katika hali ya kutenda. "watu pamoja na mimi tunauona upinde wa mvua"

upinde wa mvua

mstari wa rangi wenye mwanga unaojitokeza katika mvua ambapo jua hungaa kutoka nyuma ya mtazamaji.

nitakumbuka agano langu

Hii haimaanishi ya kwamba Mungu angesahau kwanza. "Nitafikiria juu ya agano langu"

yangu na ninyi

Neno "ninyi" ni wingi. Mungu anazungumza na Nuhu na wana wa Nuhu.

kila kiumbe hai cha wote mwenye mwili

"kila aina na kiumbe hai"

mwenye mwili

Maana zaweza kuwa 1) binadamu wote au 2) wenye viumbe wote wenye mwili, kujumlisha binadamu na wanyama.

Genesis 9:16

Maelezo ya Jumla:

Mungu anaendelea kuzungumza na Nuhu na wanawe.

ili kukumbuka

"ili kwamba nikumbuke" au "ili kwamba nitafikiria juu ya"

kati ya Mungu na kila kiumbe

Mungu anazungumza hapa. "kati yangu na kila kiumbe hai"

kila kiumbe hai cha wote wenye mwili

"kila aina ya kiumbe hai"

Kisha Mungu akamwambia Nuhu

Mungu alikuwa tayari anazungumza na Nuhu. Msemo huu unaweka alama ya sehemu ya mwisho ya kile Mngu alichokuwa akisema. "Mungu alimalizia kwa kusema kwa Nuhu" au "Kwa hiyo Mungu akasema kwa Nuhu"

Genesis 9:18

Maelezo ya Jumla

Mistari ya 18-19 inatambulisha wana watatu wa Nuhu, ambao watakuwa sehemu muhimu katika simulizi ifuatayo.

baba

Hamu alikuwa baba wa Kaanani wa halisi.

Genesis 9:20

mkulima

"mtu wa ardhi"

akalewa

"alikunywa divai nyingi sana"

uchi

Maandishi haisemi jinsi gani mwili wa Nuhu ulikuwa uchi alipokuwa amelala kalewa. Mapokeo ya wanawe yalionyesha ya kwamba ilikuwa suala la aibu.

Genesis 9:22

baba yake

Hii ina maana ya Nuhu.

Genesis 9:24

Maelezo ya Jumla:

Katika mistari ya 25-27 Nuhu anatamka laana juu ya mwana wa Hamu na baraka juu ya ndugu za hamu. Kile alichokisema Nuhu juu yao pia iliwahusu uzao wao.

Maelezo ya Jumla:

Misemo tofauti katika mistari hii inakusudiwa kuonyesha ya kwamba hii ilikuwa shairi.

alipozinduka kutoka katika ulevi wake

"akawa mtulivu"

mtoto wake mdogo

Hii ina maana ya Hamu. "mwanawe mdogo, Hamu"

Alaaniwe Kanaani

"Ninakulaani Kaanani" au "Na mambo mabaya yafanyike kwako Kaanani"

Kanaani

Huyu alikuwa mmoja wa wana wa Hamu. "mwana wa Hamu Kaanani"

mtumishi kwa watumishi wa ndugu zake

"mtumishi wa chini wa kaka zake" au "mtumishi mwenye umuhimu wa chini kabisa kati ya ndugu zake"

ndugu zake

Hii inaweza kumaanisha ndugu zake Kaanani au ndugu zake kwa ujumla.

Genesis 9:26

Maelezo ya Jumla:

Hii ni shairi.

Yahwe , Mungu wa Shemu, abarikiwe

"Yahwe na asifiwe, Mungu wa Shemu" au "Yahwe, Mungu wa Shemu, anastahili sifa" au "Ninamsifu Yahwe, Mungu wa Shemu"

Kanaani na awe mtumishi wake

"Na Kaanani awe mtumishi wa Shemu". Hii inajumlisha uzao wa Kaanani na Shemu.

Mungu na apanue mipaka ya Yafethi

Maana zaweza kuwa 1) "Mungu na afanya mipaka ya Yafethi mikubwa" au 2) "Mungu na asababishe Yafethi kuwa na uzao mwingi"

na afanye makazi yake katika hema za Shemu

"na mfanye aishi kwa amani na Shemu". Hii inajumlisha uzao wa Yafethi na Shemu.

Kanaani na awe mtumishi wake

"Na Kaanani awe mtumishi wa Yafethi". Hii inajumlisha uzao wa Kaanani na Yafethi.

Genesis 10

Genesis 10:1

Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya wana wa Nuhu

"Hii ni habari ya wana wa Nuhu." Sentensi hii inatambulisha habari ya vizazi vya Nuhu katika Mwanzo 10:1-11:9

Genesis 10:2

Kutoka kwa hawa watu wa pwani waligawanyika na

"Wana wa yafethi na vizazi vyake waligawanyika na kuhamia pwani na visiwani"

watu wa pwani

Hii ina maana ya watu waliokuwa wakiishi kando ya pwani na visiwani.

ardhi zao

"makazi yao". Hizi ni sehemu ambazo watu waliohama waliishi.

kila mtu na lugha yake

"Kila kundi la watu lilizungumza lugha yake" au " Makundi ya watu walijigawa kulingana na lugha zao"

Genesis 10:6

Misraimu

Misraimu ni jina la Kihebrania la "Misri".

Genesis 10:8

hodari

Maana zaweza kuwa 1) "hodari mwenye nguvu" au 2) "mwanamume mwenye nguvu" au 3) "mtawala mwenye uwezo".

mbele za Yahwe

Maana zaweza kuwa 1) "machoni pa Yahwe" au 2) "kwa msaada wa Yahwe"

Hii ndiyo sababu hunenwa

Hii inatambulisha methali. Lugha yako yaweza tambulisha methali na misemo kwa namna tofauti. "Hii ni sababu watu husema"

Miji ya kwanza

Maana zaweza kuwa 1) miji ya kwanza aliyoijenga au 2) miji muhimu.

Genesis 10:11

alikwenda Ashuru

Nimrodi alikwenda Ashuru

Misraimu akawa

orodha ya vizazi vya Nuhu inaendelea.

Misraimu

Misraimu alikuwa mmoja wa wana wa Hamu. Vizazi vyake vikawa watu wa Misri. Misraimu ni jina la Kihebrania la Misri.

Genesis 10:15

Myebusi ... Mwamori ... Mgirgashi

Majina haya yana maana ya makundi makubwa ya watu walioshuka kutoka Kanaani.

Genesis 10:19

mpaka

"eneo" au "mpaka wa eneo"

ulianzia Sidoni, katika mwelekeo wa Gerari, hata Gaza

Mwelekeo wa kusini waweza elezwa wazi kama itahitajika. "Kutoka mji wa Sidoni magharibi hata mji wa Gaza, ambao uko karibu na Gerari"

na kama kuelekea Sodoma, Gomora, Adma, na Seboimu hata Lasha

Mwelekeo ni "mashariki" au "bara" inaweza kuelezwa wazi kama itahitajika. "kisha mashariki mwa miji ya Sodoma, Gomora, Adma na Seboimu, hata Lasha"

Hawa walikuwa wana wa Hamu

Neno "hawa" lina maana ya watu na makundi ya watu waliorodhoshwa katika mistari ya 10:6

kwa lugha zao

"waligawanyika kulingana na lugha zao tofauti"

katika ardhi zao

"katika makazi yao"

Genesis 10:24

Arfaksadi

Arfaksadi alikuwa mmoja wa wana wa Shemu.

Pelegi

Jina Pelegi lina maana ya "mgawanyiko"

nchi iligawanyika

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "watu wa duniani walijigawa wenyewe" au "watu wa duniani waligawanyika kati yao" au "Mungu aligawanya watu wa duniani"

Genesis 10:26

Yoktani

Yoktani alikuwa mmoja wa wana wa kiume wa Eberi.

Hawa

Hapa "hawa" ina maana ya wana wa kiume wa Yoktani.

Genesis 10:30

Mpaka wao

"ardhi walioitawala" au "ardhi walipoishi"

Hawa walikuwa wana wa Shemu

Neno "hawa" ina maana ya vizazi vya Shemu.

Genesis 10:32

Hizi zilikuwa koo

Hii inarudi nyuma kwa watu wote waliorodheshwa katika 10:1

kulingana na

"imeorodheshwa kwa"

kwa hawa mataifa yaligawanyika na kwenda juu ya nchi

"kutoka kwa koo hizi mataifa yaligawanyika na kusambaa nchini kote" au "Koo hizi ziligawanyika baina yao na kuunda mataifa ya dunia"

baada ya gharika

Hii inaweza kuelezwa dhahiri au kwa uwazi zaidi. "baada ya gharika kuangamiza nchi"

Genesis 11

Genesis 11:1

Sasa

Neno hili linaonyesha kuwa mwandishi anaanza sehemu mpya ya simulizi.

nchi yote

watu wote juu ya nchi

inatumia lugha moja na ilikua na usemi mmoja

Misemo hii miwili ina maana moja na inasisitiza ya kwamba watu wote walizungumza lugha moja.

waliposafiri

"walihama" au "sogea pande zote"

upande wa mashariki

Yawezekana maana ni 1) "mashariki" au 2) "kutoka mashariki" au 3) "kuelekea mashariki". Chaguo linalofaa ni "mashariki" kwa sababu Shinari ipo upande wa mashariki ambapo wasomi wanaamini safina ilikuja kutulia.

wakakaa

waliacha kusogea kutoka sehemu moja hadi nyingine na wakaanza kuishi sehemu moja.

Genesis 11:3

haya njooni

"haya njooni"

tuyachome kikamilifu

Watu hutengeneza matofali kwa udongo na kuyachoma ndani ya joko la moto sana ili yawe magumu na imara.

lami

kimiminiko kinene, kinachonata, cheusi kinachotoka ardhini.

chokaa

hiki ni kiini kinene kinachoundwa kwa unga wa ndimu, udongo, mchanga, na maji inayotumika kufanya mawe au matofali kugandamana.

tujifanyie jina

"tujifanyie sifa yetu kuwa kubwa"

jina

"sifa"

tutatawanyika

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "tutajigawanya baina yetu na kuishi sehemu tofauti"

Genesis 11:5

wazao wa Ibrahimu

"watu"

akashuka

Habari kuhusu mahali aliposhuka inaweza kuwekwa wazi. "akashuka kutoka mbinguni". Hii haielezi jinsi gani alishuka kutoka mbinguni.

kuona

"angalia kwa makini" au "kutazama kwa makini zaidi"

watu hawa ni taifa moja na lugha moja

Watu wote walikuwa katika kundi moja kubwa na wote walizungumza lugha moja.

wanaanza kufanya hivi

Yawezekana maana kuwa 1) "wameaanza kufanya hivi" ikimaanisha ya kwamba wameanza kujenga mnara lakini haijakamilika au 2)"hili ni jambo la kwanza walilofanya", ikimaanisha ya kwamba katika siku za usoni watafanya mambo makubwa zaidi.

halitashindikana jambo watakalo kusudia kulifanya

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "kila jambo wanalikusudia kufanya litawezekana kwao"

Haya! Njooni

"haya! njooni"

tushuke

Neno "tushuke" ni wingi ingawa ina maana ya Mungu. Tafsiri zingine husema "na nishuke" au "nitashuka"

tuvuruge lugha yao

Hii ina maana ya kwamba Yahwe angesababisha watu wote wa nchi kukoma kuzungumza lugha moja. "kuchanganya lugha yao"

ili kwamba wasielewane

Hii ilikuwa lengo la kuchanganya lugha yao. "ili kwamba wasiweze kuelewa kile mwingine anachokisema"

Genesis 11:8

kutoka pale

"kutoka katika mji"

jina lake ukaitwa Babeli, kwa sababu hapo Yahwe alivuruga

Jina la "Babeli" linaonekana kama neno lenye maana ya "kuchanganyikiwa"

alivuruga lugha ya nchi yote

Ina maana ya kwamba Yahwe alisababisha watu wote katika nchi kutozungumza lugha moja. "alichanganya lugha ya nchi yote"

Genesis 11:10

Taarifa ya jumla

Sura iliyosalia inaorodhesha mtiririko wa vizazi vya Shemu mpaka vya Abramu.

Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Shemu

Sentensi hii inaanza orodha ya vizazi vya Shemu.

gharika

Hii ilikuwa gharika kutoka kipindi cha Nuhu ambapo watu walikuwa waovu sana mpaka Mungu akatuma gharika nchi yote kufunika nchi.

akawa baba wa Alfaksadi

"akapata mwana wake wa kiume Alfaksadi" au "mwana wake wa kiume Alfaksadi alizaliwa"

Alfaksadi

jina la mwanamume

mia moja ... miwili ... mia tano

Watafsiri wanaweza kuandika maneno au namba "100", "2", and "500".

Genesis 11:12

akawa baba wa Shela

"mwana wa kiume wake Shela alizaliwa"

Shela

jina la mwanamume

Genesis 11:14

Taarifa ya Jumla:

Kumbukumbu katika Mwanzo 11:12-25 zilikuwa na mfumo huo huo.

Genesis 11:16

Taarifa ya Jumla:

Kumbukumbu katika Mwanzo 11:12-25 zilikuwa na mfumo huo huo.

Genesis 11:18

Taarifa ya Jumla:

Kumbukumbu katika Mwanzo 11:12-25 zilikuwa na mfumo huo huo.

Genesis 11:20

Taarifa ya Jumla:

Kumbukumbu katika Mwanzo 11:12-25 zilikuwa na mfumo huo huo.

Genesis 11:22

Taarifa ya Jumla:

Kumbukumbu katika Mwanzo 11:12-25 zilikuwa na mfumo huo huo.

Genesis 11:24

Taarifa ya Jumla:

Kumbukumbu katika Mwanzo 11:12-25 zilikuwa na mfumo huo huo.

Abramu, Nahori, na Harani

Hatujui mpangilio wa kuzaliwa kwa watoto wake.

Genesis 11:27

Hivi ndivyo vilikuwa vizazi vya Tera

Sentensi hii inatambulisha habari ya vizazi vya Tera. Mwanzo 11:27-25:11 unazungumzia kuhusu vizazi vya Tera, mahsusi mwanae Abrahamu. "Hii ni habari ya vizazi vya Tera"

Harani akafa machoni pa baba yake Tera

Hii ina maana ya kwamba Harani alikufa wakati baba yake akiwa hai. "Harani alikufa wakati baba yake, Tera, alipokuwa naye"

Genesis 11:29

wakajitwalia wake

"akaoa wake"

Iska

hili ni jina la kike

Sasa

Neno hili linatumiwa kutambulisha habari mpya kuhusu Sarai ambayo itakuwa muhimu baadae katika sura.

tasa

Lugha hii inaelezea mwanamke ambaye kimwili hawezi kutunga mimba au kuzaa mtoto.

Genesis 11:31

akamtwaa

Hapa neno "mwana wa" lina maana ya Tera.

Sarai mkwewe, mke wa mwanawe Abramu

mkwewe, mwanawe mke wa Abramu - "mkwe wa Sarai, ambaye alikuwa mke wa mwanawe Abramu.

Harani ... Harani

Haya ni majina mawili tofauti na yanaandikwa tofauti Kihebrania. Moja lina maana ya mtu na lingine lina maana ya mji.

Genesis 12

Genesis 12:1

Sasa

Neno hili linatumika kuweka alama sehemu mpya ya simulizi.

Nenda utoke katika nchi yako, na toka kwa ndugu zako

"Nenda kutoka nchini kwako, kutoka katika familia yako"

Nitakufanya uwe taifa kubwa

Hapa "nitakufanya" ni umoja na ina maana ya Abramu, lakini Abramu anawakilisha vizazi vyake. "Nitaanzisha taifa kubwa kupitia kwako" au "Nitawafanya vizazi vyako kuwa taifa kubwa"

na kulifanya jina lako kuwa kubwa

Neno "jina" linawakilisha sifa ya mtu. "na kukufanya uwe maarufu"

na utafanyika baraka

neno "jina" linawakilisha sifa ya mtu. "na kukufanya uwe maarufu"

asiye kuheshimu nita mlaani

"Nitamlaani yeyote atakayekutendea jambo kwa njia ya aibu" au "iwapo kuna mtu atakayekutendea jambo lisilofaa, nitamlaani"

Kupitia kwako familia zote za nchi zitabarikiwa

Hii inaweza kufanywa katika hali ya kutenda. "Nitabariki familia za nchi kupitia kwako"

Kupitia kwako

"Kwa sababu yako" au "Kwa sababu nimekubariki"

Genesis 12:4

walivyomiliki

Hii inajumlisha wanyama na mali isiyokuwa na uhai

Watu ambao wamewapata

Maana yaweza kuwa 1) "watumwa ambao wamewakusanya" au 2) "watu ambao wamewakusanya kuwa pamoja nao"

Genesis 12:6

Abramu akapitia katikati ya nchi

Ni jina la Abramu pekee linatajwa kwa sababu alikuwa kichwa cha familia. Mungu alimpatia amri ya kuchukua familia yake na kwenda kule. "Kwa hiyo Abramu na familia yake walikwenda katikati ya nchi"

nchi

"nchi ya Kanaani"

mwaloni wa More

Yawezekana More ilikuwa jina ya sehemu

Yahwe aliyemtokea Abramu

"Yahwe, kwa sababu alimtokea"

Genesis 12:8

alipiga hema yake

Abramu alikuwa na watu wengi pamoja naye alipokuwa akisafiri. Watu waliokuwa wakihama kutoka sehemu moja hadi nyingine waliishi ndani ya mahema. "walitengeneza mahema yao"

kuliitia jina la Yahwe

"waliomba kwa jina la Yahwe" au "kumuabudu Yahwe"

Kisha Abram akaendelea kusafiri

"Kisha Abramu alichukua hema lake na kuendelea na safari"

upande wa Negebu

"kuelekea eneo la Negebu" au "kuelekea kusini" au "kusini ya jangwa la Negebu"

Genesis 12:10

Kulikuwa na njaa

Mazao hayakuota vizuri msimu huo.

katika nchi

"katika eneo" au "katika nchi ambapo Abramu alikuwa akiishi"

akaenda chini kuingia

Maana zaweza kuwa 1) "alikwenda kusini zaidi" au 2) "aliondoka mbali na Kaanani kuingia". Ingependeza kutafsiri kwa kutumia maneno ya kawaida ya kutoka eneo la juu kuelekea eneo la chini.

wataniua mimi ... wewe hai

Sababu watakayomuua Abramu inaweza kufanywa wazi. "wataniua ili kwamba wakuoe"

ili kwamba niwe salama kwa sababu yako

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ili kwamba, kwa sababu yako, hawataniua mimi"

Genesis 12:14

Ikawa kwamba

Maana zaweza kuwa 1) Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya wapi tukio linaanza, na kama lugha yako ina namna ya kufanya hivi basi tumia njia hiyo, au 2) "Na hivyo ndivyo kilichotokea"

Wakuu wa Farao wakamuona

"Wakuu wa Farao walimwona Sarai" au "wakuu wa Farao walimwona"

mwanamke akachukuliwa kupelekwa nyumbani mwa Farao

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Farao akamchukua mpaka nyumbani kwake" au "Farao aliwaamuru askari wake kumpeleka nyumbani kwake"

mwanamke

Sarai

nyumbani mwa Farao

Maana zaweza kuwa 1)"Familia ya Farao", yaani kama mke au 2) "Nyumba ya Farao" au "Hekalu la Farao" ni tasifida ya Farao kumfanya awe mmoja wa wake zake.

kwa ajili yake

"kwa ajili ya Sarai" au "kwa sababu yake"

Genesis 12:17

kwa sababau ya Sarai, mke wa Abramu

Hii inaweza kufanywa kwa uwazi zaidi. "Kwa kuwa Farao alitaka kumchua Sarai , mke wa Abramu, aweze kuwa mke wake mwenyewe"

Farao akamwita Abramu

"Farao akamuita Abramu" au "Farao akamuamuru Abramu kuja kwake"

Nini hiki ambacho umenifanyia?

Farao alitumia lugha hii ya balagha kuonyesha jinsi gani alivyokasirika juu ya kile Abramu alichomfanyia. Inaweza kuelezeka kwa namna ya mshangao. "Umedanya jambo baya kwangu!"

Kisha Farao akatoa amri kwa watu wake kuhusiana naye

"Kisha Farao akawaongoza wakuu wake kuhusu Abramu"

na wakamuondoa, yeye pamoja na mke wake na vyote alivyokuwa navyo

"na wakuu wakamfukuza Abramu kutoka kwa Farao, pamoja na mke wake na alivyokuwa navyo"

Genesis 13

Genesis 13:1

akaondoka kutoka

"kwenda" au "kuondoka kutoka"

akaenda Negebu

Negebu ilikuwa ni eneo la jangwa kusini mwa Kanaani, magharibi mwa Misri. Hii inaweza kufanywa kwa uwazi. "akarudi katika jangwa la Negebu"

Abram alikuwa tajiri wa wanyama, fedha na dhahabu

"Abramu alikuwa na wanyama wengi, fedha nyingi na dhahabu nyingi"

wanyama

"mifugo" au "ng'ombe"

Genesis 13:3

Aliendelea na safari yake

Abramu na familia yake walisafiri kwa hatua, kwenda kutoka sehemu hadi sehemu. Hii inaweza kufanywa wazi. "Waliendelea na safari yao"

mahali ambapo hema yake ilikuwa tangu mwanzo

Watafsiri wanaweza kuweka maandishi machache yanayosema "Tazama Mwanzo 12:8." Muda wa safari yake unaweza kuwekwa wazi. "katika eneo alipotenga hema lake kabla hajakwenda Misri"

akaliitia jina la Yahwe

"aliomba katika jina la Yahwe" au"alimuabudu Yahwe"

Genesis 13:5

Sasa

Neno hili linatumika kuonyesha kitakachofuatia ni taarifa ya nyuma kumsaidia msomaji kuelewa matukio yatakayofuata.

Nchi haikuwatosha wote

Hapakuwa na ardhi ya kutosha ya malisho na maji kwa ajili ya wanyama wao.

mali zao

Hii inajumuisha mifugo, ambayo inahitaji malisho na maji.

hawakuweza kukaa pamoja

"hawakuweza kuishi pamoja"

Wakanaani pamoja na Waperizi walikuwa wakiishi katika nchi ile wakati huo

Hii ni sababu nyingine ya nchi kutoweza kuwahimili wote.

Genesis 13:8

Pasiwe na ugomvi kati yako na mimi,

"Tusigombane"

ugomvi

"chuki" au "ugomvi" au "malumbano"

na kati ya wachunga wanyama wako na wachunga wanyama wangu

"na tuwazuie wanaume wanaochunga wanyama wetu kulumbana"

licha ya hayo sisi ni familia

"kwa sababu sisi ni familia"

familia

"ndugu" au "jamaa". Lutu alikuwa mpwa wa Abramu.

Je nchi hii yote haiko mbele yako?

Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa katika hali ya chanya. "nchi nzima ipo wazi kwa matumizi yako"

Nenda na ujitenge na mimi

Abrahamu alizungumza kwa huruma na Lutu na kumtia moyo afanye jambo litakalowasaidia wote. "Tugawanyike".

Ikiwa utakwenda kulia, mimi nitakwenda kushoto

Maana zaweza kuwa 1) "ukienda njia moja, basi na mimi nitaenda njia nyingine" au 2) "ukienda kaskazini, nitaenda kusini." Abramu alimruhusu Lutu kuchagua sehemu ya nchi aliyoitaka, na Abramu angechukua kile kilichobaki.

Genesis 13:10

nchi yote tambarare ya Yorodani

Hii ina maana ya eneo la jumla la mto Yordani.

ilikuwa na maji kila mahali

"ilikuwa na maji mengi"

kama vile bustani ya Yahwe, na kama nchi ya Misri

"kama bustani ya Yahwe au kama nchi ya Misri". Haya yalikuwa maeneo mawili tofauti.

bustani ya Yahwe

Hili ni jina lingine kwa bustani ya Edeni.

bustani

Hii yaweza kuwa shamba la miti ya matunda au eneo lenye kila aina ya miti.

Hii ilikuwa ni kabla Yahwe hajaiangamiza Sodoma na Gomora

Hii inatazamia jambo litakalotokea baadae. Hapa ni muhimu kwa sababu inaeleza kwa nini Lutu alikaa katika eneo ambalo baadae halikuwa na mbolea.

ndugu

"ndugu wa karibu" au "familia". Hii ina maana ya Lutu na Abramu pamoja na nyumba zao.

Genesis 13:12

akaishi

"akatulia" au "akakaa"

nchi ya Kanaani

"nchi ya watu wa Kanaani"

Akatandaza hema zake hadi Sodoma

Maana zaweza kuwa 1) "alitandaza mahema yake karibu na Sodoma" au 2) "Alisogeza mahema yake kuzunguka eneo lililofika hadi Sodoma".

Genesis 13:14

baada ya Lutu kuondoka kwake

"baada ya Lutu kumuacha Abrahamu"

Genesis 13:16

tembea katika urefu na upana wa nchi hii,

"kutembea tembea juu ya ardhi nzima"

Mamre

Hii ilikuwa jina la mwanamume aliyemiliki miti ya mwaloni.

Hebroni

jina la sehemu

madhabahu ya Yahwe

"dhabahu la kumuabudu Yahwe"

Genesis 14

Genesis 14:1

Taarifa ya Jumla:

Maeneno katika 14:1 yote ni miji inayojitegemea

ikaja kuwa

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

katika siku

"katika muda wa"

walifanya vita

"walienda vitani" au "walianzisha vita" au "walijiandaa kwa vita"

Genesis 14:3

Hawa wafalme watano wa mwisho waliungana pamoja

Taarifa ya kwamba majeshi yao walikuwa pamoja nao inaweza kuwekwa wazi. "Wafalme hawa watano wa nyuma na majeshi yao waliungana"

miaka kumi na mbili walimtumikia

Matukio katika mistari ya 4-7 yalitokea kabla ya mstari wa 3. Lugha yakoinaweza kuwa na namna ya kuonyesha hivi.

walimtumikia Kedorlaoma

Inawezekana walitakiwa kumlipa kodi na kumtumikia jeshini. "walikuwa chini ya utawala wa Kedorlaoma"

waliasi

"walikataa kumtumikia" au "walisitisha kumtumika"

walikuja na kuwashambulia

Walifanya hivi kwa sababu wafalme wengine waliasi.

Warefai ... Wazuzi ... Waemi ... Wahori

Haya ni majina ya makundi ya watu.

Ashteroth Karnaimu ... Hamu ... Shawe Kiriathaimu ... Seiri ...El Parani

Haya ni majina ya sehemu.

El Parani iliyo karibu na jangwa

Huu msemo unasaidia wasomaji kuelewa El parani ilikuwa wapi. Inaweza kutafsiriwa katika sentensi tofauti kama italazimu. "El Parani. El Parani ipo karibu na jangwa"

Genesis 14:7

Taarifa ya Jumla:

Mistari ya 8 na 9 inarudia kile kilichosemwa katika 14:3 na kuendelea kueleza yaliyojiri baada ya wafalme kukutana pamoja kupigana.

wakarudi wakaja

Neno "wakarudi" lina maana ya wafalme wanne wageni ambao walikuwa wakishambulia eneo la Kanaani. Majina yao yalikuwa Amrafeli, Arioko, Kadorlaoma na Tidali. "wakageuka na kuondoka"

Waamori ambao waliishi Hasasoni Tamari

Msemo huu unaelezea juu ya watu wa Waamori walioshindwa. Hawa walikuwa Waamori wengine walioishi katika maeneno mengine.

na mfalme wa Bela (pia ikiitwa Soari)

Mji wa Bela pia ulikuwa unaitwa Soari. Taarifa hii inaweza kuwekwa mwishoni mwa sentensi. "na mfalme wa Bela akaondoka na kujiandaa kwa vita. Bela pia inaitwa Soari.

kujiandaa kwa vita

"kujiunga vitani" au "kuanza mistari ya vita" Baadhi ya watafsiri wanaweza kusema kuwa majeshi yalipigana.

afme wanne dhidi ya wale watano

Kwa kuwa wafalme watano waliorodheshwa kwanza, baadhi ya lugha inaweza kutafsiri hii kama "wafalme watano dhidi ya wanne".

Genesis 14:10

Sasa

Neno hili linatambulisha taarifa ya nyuma kuhusu bonde la Sidimu. Lugha yako inaweza kuwa na njia nyingine ya kutambulisha taarifa hii ya nyuma.

lilikuwa limejaa mashimo ya lami

"ilikuwa na mashimo ya lami mengi". Haya yalikuwa mashimo katika ardhi ambayo yalikuwa na lami ndani mwao.

lami

kimiminiko kinene, kinachonata, cheusi kinachotoka ardhini.

wafalme wa Sodoma na Gomora

Huu ni usemi mwingine kwa ajili ya wafalme na majeshi yao. "wafalme wa Sodoma na Gomora na majeshi yao"

wakaanguka pale

Maana zaweza kuwa 1) baadhi ya wanajeshi wao walianguka ndani ya mashimo ya lami au 2) wafalme wenyewe walianguka ndani ya mashimo ya lami. Kwa kuwa 14:17 unasema ya kwamba mfalme wa Sodoma alikwenda kukutana na Abramu, maana ya kwanza yaweza kuwa sahihi zaidi.

Wale waliosalia

"Wale ambao hawakufa vitani na hawakuanguka ndani ya mashimo"

adui

Hii ina maana ya mfalme Kedorlaoma na wafalme wengine na majeshi yao aliokuwa nao waliokuwa wakishambulia Sodoma na Gomora.

mali zote za Sodoma na Gomora

Maneno "Sodoma" na "Gomora" ni lugha nyingine kwa ajili ya watu walioishi katika miji ile. "utajiri wa watu wa Sodoma na Gomora" au "mali za watu wa Sodoma na Gomora"

vyakula vyao vyote

"chakula na vinywaji vyao"

wakaenda zao

"wakaenda njia zao"

wakamchukua pia Lutu, mtoto wa ndugu yake na Abramu ambaye aliishi Sodoma, pamoja na mali zake zote

Misemo ya "mwana wa kaka wa Abramu" na "aliyekuwa akiishi Sodoma" unamkumbusha msomaji juu ya mambo yaliyoandikwa mapema kuhus Lutu. "walimchukua Lutu pia, pamoja na na mali zake zote. Lutu alikuwa mwana wa kaka wa Abramu na alikuwa akiishi Sodoma kwa kipindi hicho"

Genesis 14:13

Mmoja ambaye alitoroka alikuja

"Mwanamume alitoroka vitani na kuja"

Alikuwa anaishi

"Abramu alikuwa anaishi" Hii inatambulisha taarifa ya nyuma.

walikuwa washirika wa Abram

"walikuwa washirika wa mkataba na Abramu" au "alikuwa na makubaliano ya amani na Abramu"

ndugu yake

Hii inahusu mpwa wa Abramu Lutu

wanaume waliofunzwa

"wanamume waliofunzwa kupigana"

wanaume waliozaliwa nyumbani mwake

"wanamume waliozaliwa nyumbani mwa Abramu". Walikuwa watoto wa watumishi wa Abramu.

akawafukuza

"akawafukuza"

Dani

Huu ni mji wa kaskazini wa Kanaani, mbali ya kambi ya Abramu.

Genesis 14:15

Akawagawanya watu wake dhidi yao usiku na kuwavamia

Yawezekana hii ina maana ya mipango ya vita. "Abramu aliwagawa wanamume katika makundi kadhaa, na wakawashambulia maadui zao katika pande zote"

mali zote

Hii ina maana ya vitu ambavyo maadui waliiba kutoka miji ya Sodoma na Gomora.

mali zake

"na mali za Lutu ambazo maadui waliiba kutoka kwa Lutu"

pamoja na wanawake na watu wengine

"pamoja na wanawake na watu wengine ambao wafalme wanne waliwakamata"

Genesis 14:17

kurudi

Taarifa inayodokezwa kuhusu wapi alipokuwa anarudi inaweza kuwekwa wazi. "alirudi hadi pale alipokuwa akiishi"

Melkizedeki, mfalme wa Salemu

Hii ni mara ya kwanza mfalme huyu anatajwa.

mkate na divai

Watu hula mkate na divai mara kwa mara.

Genesis 14:19

Alimbariki

Mfalme Melkizedeki alimbariki Abramu.

Abarikiwea Abramu na Mungu aliye juu sana, muumba wa mbingu na nchi

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mungu aliye Juu Sana, Muumba wa mbingu na nchi, ambariki Abramu"

mbingu

Hii ina maana ya sehemu ambayo Mungu huishi.

Mungu aliye juu sana, ambaye amekupatia

"Mungu aliye juu sana, kwa sababu amekupatia". Msemo unaoanza na "ambaye amekupatia" unatueleza jambo zaidi kuhusu Mungu aliye juu sana.

Abarikiwe Mungu aliye juu sana

Hii ni njia ya kumsifu Mungu.

mikono yako

"ndani ya utawala wako" au "ndani ya uwezo yako"

Genesis 14:21

Nipatie watu

Msemo "watu" unaweza kuwa na maana ya watu wa Sodoma ambao maadui waliwakamata. Abramu aliwaokoa alipomuokoa Lutu.

Nimeinua juu mkono wangu

Hii ina maana "nimetoa kiapo" au "nimefanya ahadi".

Sitachukua chochote isipokuwa kile ambacho vijana wamekula

"Ninachukua kutoka kwako kile tu vijana wangu walishakwisha kula". Abramu alikuwa akikataa kupokea chochote kwa ajili yake, lakini alikiri kuwa wanajeshi wake wamekula sehemu ya akiba wakati wa safari ya kurudi Sodoma baada ya vita.

sehemu za watu waliokwenda nami.

Maana kamili ya kauli hii yawezwa kuwekwa wazi. "sehemu ya mali iliyokombolewa iliyokuwa ya wanamume walionisaidia kurudi"

Aneri, Eskoli, na Mamre

Hawa ni washirika wa Abramu (14:13). Kwa kuwa walikuwa washirika wa Abramu walipigana vita pamoja naye. Maana kamili ya kauli inaweza kufanywa wazi. "washirika wangu Aneri, Eskoli na Mamre"

Genesis 15

Genesis 15:1

Baada ya mambo haya

"Mambo haya" ina maana ya pale ambapo wafalme walipigana na Abramu akamuokoa Lutu.

neno la Yahwe likamjia

Lahaja hii ina maana ya Yahwe akazungumza. "Yahwe alizunguza ujumbe wake"

neno la Yahwe

Hapa "neno" inawakilisha ujumbe wa Yahwe. "ujumbe wa Yahwe"

ngao ... thawabu

Mungu alitumia sitiari hizi mbili kumwambia Abramu juu ya tabia yake na uhusiano wake na Abramu.

mimi ni ngao yako

Wanajeshi hutumia ngao kujilinda kwa maadui zao. "Nitakulinda kama ngao" au "Mimi ni ngao yako kukulinda"

thawabu

"malipo". Hii ina maana ya malipo yanayostahili kwa mtu. Maana mbili zaweza kuwa 1) "Mimi ni yote unayohitaji" au 2) "Nitakupa yote unayohitaji".

Abram akasema, "Kwakuwa hujanipatia

"Abramu aliendelea kuzungumza na kusema, "Kwa kuwa umenipatia"

Genesis 15:4

Kisha, tazama

Neno "tazama" linasisitiza ukweli ya kwamba neno la Yahwe lilikuja kwa Abrahamu tena.

neno la Yahwe likaja

Lugha hii ina maana ya kuwa Mungu alizungumza. "Yahwe alizungumza ujumbe wake"

neno la Yahwe

Hapa "neno" linawakilisha ujumbe wa Yahwe. "Ujumbe wa Yahwe"

Mtu huyu

Hii ina maana ya Eliezeri wa Dameski.

atakaye toka katika mwili wako ndiye

"yule utakayekuwa baba yake" au "mwana wako kabisa". Mwana wa Abramu atakuwa mrithi wake.

uzihesabu nyota

"hesabu nyota"

ndivyo uzao wako utakavyokuwa

Kama vile Abramu atavyoshindwa kuhesabu nyota zote, hataweza kuhesabu uzao wake wote kwa sababu utakuwa mwingi sana.

Genesis 15:6

Akamwamini Yahwe

Hii ina maana alipokea na kuamini kile Yahwe alichosema ni kweli.

akamuhesabia jambo hili kuwa mwenye haki

"Yahwe alimhesabia imani ya Abramu kama haki" au "Yahwe alimchukulia Abramu kuwa na haki kwa sababu Abramu alimuamini"

Mimi ni Yahwe, niliye kutoa katika Uru

Yahwe alikuwa akimkumbusha Abrahamu kile alichokuwa amefanya ili Abrahamu aweze kumjua Yahwe alikuwa na nguvu kumpatia Abramu kile alichomuahidi.

kuirithi

"kukipokea" au "ili kwamba ukimiliki"

nitajua je

Abramu alikuwa akiulizia ushahidi zaidi ya kwamba Yahwe atampatia ile nchi.

Genesis 15:9

mizoga

"miili iliyokufa ya wanyama na ndege"

Abram akawafukuza

"Abramu aliwafukuza ndege". Alihakikisha ndege hawakula wanyama waliokufa.

Genesis 15:12

Abramu akalala usingizi

Hii ni lahaja. "Abrahamu alilala usingizi mzito"

giza zito na la kutisha

"giza kubwa sana lililomtisha"

ikamfunika

"ikamzunguka"

wageni

"wageni"

watatumikishwa na kuteswa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "na wamiliki wa nchi ile watawatumikisha na kuwatesa"

Genesis 15:14

Taarifa ya Jumla:

Yahwe aliendelea kuzungumza na Abramu wakati Abramu alipokuwa akiota.

Nitahukumu

Hapa "hukumu" ni lugha nyingine kwa kile kitakachotokea baada ya Mungu kutoa hukumu. "Nitaadhibu"

wataowatumikia

Maana kamili ya kauli hii inawezwa kufanywa wazi. "ambao vizazi vyako watawatumikia"

mali nyingi

Hii ni lahaja. "mali nyingi" au "utajiri mkubwa"

utakwenda kwa baba zako

Hii ni njia ya upole ya kusema "utakufa"

baba

Neno "baba" lina maana sawa na mababu. "mababu"

utazikwa katika uzee mwema

"utakuwa mzee sana utakapokufa na familia yako itazika mwili wako"

Katika kizazi cha nne

Hapa kizazi kimoja kina maana ya urefu wa miaka 100. "Baada ya miaka mia nne"

watakuja tena hapa

"vizazi vyako watakuja hapa tena". Vizazi vya Abrahamu vitakuja katika nchi ampabo Abramu alikuwa akiishi, nchi ambayo Yahwe aliahidi kumpatia.

haujafikia mwisho wake

"haijakamilika" au "itakuwa mbaya zaidi kabla sijawaadhibu"

Genesis 15:17

tazama

Neno "tazama" hapa linatuamsha kuwa makini kwa taarifa ya kushangaza inayofuata.

moshi wenye moto na miali ya mwanga ilipita kati ya vile vipande

Mungu alifanya hivi kumuonyesha Abramu ya kuwa alikuwa akifanya agano na yeye.

ilipita kati ya vile vipande

"ilipita katikati ya mistari miwili ya vipande vya wanyama"

agano

Katika agano hili Mungu alimuahidi kumbariki Abramu, naye ataendelea kumbariki ikiwa Abramu ataendelea kumfuata yeye.

Ninatoa nchi hii

Kwa kusema hivi, Mungu alikuwa akiwapa uzao wa Abramu nchi. Mungu alikuwa akifanya hivi, lakini uzao hawakuweza kwenda katika nchi hadi baada ya miaka mingi baadae.

mto mkuu, Frati

"mto mkubwa, Frati". Hizi ni njia mbili zinazoelezea mto mmoja.

Mkeni , Mkenizi, na Mkadmoni, Mhiti, Mperizi, Mrefai, Mwamori, Mkanaani, Mgirgashi, na Myebusi.

Haya ni majina ya makundi ya watu ambao waliishi katika nchi. Mungu angeruhusu uzao wa Abrahamu kuwashinda watu hawa na kuchukua nchi yao.

Genesis 16

Genesis 16:1

Sasa

Neno hili linatumika kutambulisha sehemu mpya ya simulizi na taarifa ya nyuma kuhusu Sarai.

mtumishi wa kike

"mtumwa wa kike". Mtumwa wa namna hii alikuwa akimtumikia mwanamke wa nyumbani.

kutopata watoto

"kutoweza kuzaa watoto"

niweze kupata watoto kupitia yeye

"Nitajenga familia yangu kupitia kwake"

Abram akasikiliza sauti ya Sarai

"Abramu alifanya kile Sarai alichosema"

akamdharau bibi yake

"alimdharau bibi yake" au "alifikiria alikuwa na thamani zaidi ya bibi yake"

bibi yake

Hapa ina maana ya Sarai. Bibi alikuwa na uwezo juu ya mtumwa wake. "mmiliki wake" au "Sarai"

Genesis 16:5

Jambo hili baya kwangu

"Udhalimu huu dhidi yangu"

ni kwa sababu yako

"ni wajibu wako" au "ni kosa lako"

Nilimtoa mtumishi wangu wa kike katika kumbatio lako

Sarai alitumia neno "kumbatia" hapa kumaanisha yeye kulala naye. "Nilimpa mtumishi wangu ili uweze kulala naye"

nilidharaulika machoni pake

Hii inaweza kuwa katika hali ya kutenda. "alinichukia" au"alianza kunichukia" au "alidhani yeye ni bora zaidi yangu"

Na sasa acha Yahwe aamuwe kati yangu na wewe

"Ninataka Yahwe aseme kama hili ni kosa langu au lako" au "Nataka Yahwe kuamua nani kati yetu yupo sahihi." Msemo "aamue kati ya" una maana ya kuamua nani yuko sawa katika ugomvi kati yao"

Tazama, hapa

"Nisikilize mimi" au "Sikiliza kwa makini"

katika uwezo wako

"chini ya mamlaka yako"

Sarai akakabiliana naye kwa ukatili

"Sarai alimtendea Hajiri vibaya sana"

na akatoroka

"na Hajiri akatoroka kwa Sarai"

Genesis 16:7

Malaika wa Yahwe

Maana zinaweza kuwa 1) Yahwe alijifanya kuonekana kama malaika au 2) huyu alikuwa mmoja wa malaika wa Yahwe au 3) huyu alikuwa mjumbe maalumu kutoka kwa Mungu (baadhi ya wasomi wanadhani alikuwa Yesu). Kwa sababu msemo hauleweki vizuri, ni bora kutafsiri kama "malaika wa Yahwe" kwa kutumia neno la kawaida linalotumika kwa "malaika".

jangwa

Eneo la jangwa aliloenda lilikuwa ni nyikani. "jangwa"

Shuri

Hii ilikuwa jina ya sehemu kusini mwa Kaanani mashariki mwa Misri.

bibi yangu

Hapa ina maana ya Sarai. Bibi alikuwa na mamlaka juu ya mtumwa wake. "mmiliki wangu".

Genesis 16:9

Malaika wa Yahwe akamwambia

"Malaika wa Yahwe alimwambia Hajiri"

Malaika wa Yahwe

Maana zinaweza kuwa 1) Yahwe alijifanya kuonekana kama malaika au 2) huyu alikuwa mmoja wa malaika wa Yahwe au 3) huyu alikuwa mjumbe maalumu kutoka kwa Mungu (baadhi ya wasomi wanadhani alikuwa Yesu). Kwa sababu msemo hauleweki vizuri, ni bora kutafsiri kama "malaika wa Yahwe" kwa kutumia neno la kawaida linalotumika kwa "malaika".

bibi yako

Hapa ina maana ya Sarai. Bibi alikuwa na uwezo juu ya mtumwa wake. "mmiliki wake" au "Sarai"

Kisha Malaika wa Yahwe akamwambia, "Nita

Aliposema "Nita" alikuwa ana maana ya Yahwe.

Nitazidisha uzao wako maradufu

"Nitakupatia uzao mwingi sana"

wengi wasioweza kuhesabika

"wengi sana hadi hakuna mtu atakayeweza kuwahesabu"

Genesis 16:11

Malaika wa Yahwe

Maana zinaweza kuwa 1) Yahwe alijifanya kuonekana kama malaika au 2) huyu alikuwa mmoja wa malaika wa Yahwe au 3) huyu alikuwa mjumbe maalumu kutoka kwa Mungu (baadhi ya wasomi wanadhani alikuwa Yesu). Kwa sababu msemo hauleweki vizuri, ni bora kutafsiri kama "malaika wa Yahwe" kwa kutumia neno la kawaida linalotumika kwa "malaika".

Tazama

"Angalia" au "Sikiliza" au "Sikiliza kwa makini"

utazaa mtoto kiume

"kuzaa mtoto wa kiume"

utamwita jina lake

"utamuita jina lake". Neno "utamuita" linamlenga Hajiri.

Ishmaeli, kwa sababu Yahwe amesikia

Watafsiri wanaweza kuweka maelezo mafupi yanayosema "Jina la 'Ishmaeli' lina maana ya 'Mungu amesikia'".

mateso

Alikuwa ameteswa na mawazo na mateso.

Atakuwa punda mwitu wa mtu

Hili halikuwa tusi. Inaweza kumaanisha Ishmaeli angekuwa anajitegemea na mwenye nguvu kama punda mwitu. "Atakuwa kama punda mwitu miongoni mwa watu"

Atakuwa adui dhidi ya kila mtu

"Atakuwa adui wa kila mtu"

kila mtu atakuwa adui yake

"Kila mtu atakua adui yake"

na ataishi kando na

Hii inaweza pia kumaanisha "ataishi kwa uadui pamoja na"

ndugu

"ndugu wa karibu"

Genesis 16:13

Yahwe aliye zungumza naye

"Yahwe, kwa sababu alizungumza naye"

je ninaendelea kweli kuona, ... mimi?

Hajiri alitumia swali hili la balagha kuonyesha mshangao wake wa kuwa hai hata baada ya kukutana na Mungu. Watu walitarajia iwapo wanakutana na Mungu, wangekufa. "Ninashangaa ya kwamba bado nipo hai, ... mimi"

Kwa hiyo kisima kiliitwa Beerlahairori

Watafsiri wanaweza kuongeza maandishi yanayosema "Beerlahairori ina maana ya 'kisima cha yule anayeniona mimi"

Tazama, kiko kati ya Kadeshi na Beredi.

Neno "tazama" hapa linavuta ukweli kwamba kisima kilikuwa katika eneo ambalo mwandishi na wasomaji wake walijua. "tena, ilikuwa kati ya Kadeshi na Beredi"

Genesis 16:15

Hajiri akamzalia

Ujio wa Hajiri kwa Sarai na Abramu unajitokeza wazi. Unaweza kufanya hivi kuwa wazi. "Kwa hiyo Hajiri alirudi na kuzaa"

akamwita mwanawe, ambaye Hajiri amemzaa

"alimwita mtoto wake kwa Hajiri" au "alimuita wake na mtoto wa Hajiri"

Abram alikuwa

Hii inatambulisha taarifa ya nyuma kuhusu umri wa Abramu ambapo vitu hivi vilipotokea. Lugha inaweza kuwa na namna maalumu ya kutaja taarifa ya nyuma.

alipomzaa Ishmaeli kwa Abram

Hii inamaanisha "alimzaa mtoto wa Abramu, Ishmaeli." Lengo lipo kwa Abramu kupata mtoto.

Genesis 17

Genesis 17:1

Abram alipokuwa na umri wa miaka tisini na tisa

miaka mia tisa na tisa - Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

Mungu wa uwezo

"Mungu mwenye uweza wote" au "Mungu ambaye ana uwezo wote"

Uende mbele yangu

Kuenda ni sitiari kwa ajili ya kuishi, na "mbele yangu" au "katika uwepo wangu" hapa ni sitiari kwa ajili ya kutii. "Ishi kwa namna nayotaka uishi" au "Kunitii"

Kisha nitalithibitisha

"Iwapo utafanya hivi, basi nitathibitisha"

nitalithibitisha agano langu

"Nitatoa agano langu" au "Nitafanya agano langu"

agano

Katika agano hili Mungu anamuahidi kumbariki Abramu lakini pia anataka Abramu amutii.

nitakuzidisha sana

"nitazidisha kwa wingi idadi ya vizazi vyako" au "nitakupatia vizazi wengi sana"

Genesis 17:3

Abramu akainama uso wake hadi chini ardhini

"Abramu alijirusha uso chini ya ardhi" au "Abrahamu aliinama chini mara moja uso ukiwa ardhini." Alifanya hivi kuonyesha ya kuwa alimheshimu Mungu na angemtii.

Mimi

Mungu alitumia msemo huu kutambulisha kile alichoenda kukifanya kwa Abramu kama sehemu ya agano lake na Abramu.

tazama, agano langu liko nawe

Neno "tazama" hapa linasema ya kwamba kinachofuata ni cha uhakika: "agano langu na wewe ni la uhakika"

baba wa mataifa mengi

"baba wa idadi kubwa ya mataifa" au "yule ambaye mataifa mengi yatajiita"

Abrahamu

Watafsiri wanaweza kuongeza maandishi yafuatayo: Jina "Abramu" lina maana ya "baba aliyeinuliwa" na jina "Abrahamu" linafanana na "baba wa kundi"

Nitakufanya uwe na uzao mwingi

"Nitakusababisha uwe na vizazi vingi sana"

nitakufanya mataifa

"Nitasababisha vizazi vyako kuwa mataifa"

wafalme watatoka kwako

"miongoni mwa vizazi vyako kutakuwa na wafalme" au "baadhi ya vizazi vyako kutakuwa na wafalme"

Genesis 17:7

Taarifa ya Jumla:

Mungu anaendelea kuzungumza na Abrahamu.

katika vizazi vyao

"katika kila kizazi"

kwa agano la milele

"kama agano ambalo litadumu milele"

Mungu kwako na kwa wazao wako baada yako

"kuwa Mungu wako na vizazi vyako" au "agano"

Kanaani, kuwa miliki ya milele

"Kanaani, kama miliki ya milele" au"Kanaani, kuimiliki milele"

Genesis 17:9

nawe

Mungu anatumia msemo huu kutambulisha kile Abramu alichokuwa akielekea kufanya kama sehemu ya agano la Mungu na yeye.

ulishike agano langu

"fuata agano langu" au "heshimu agano langu" au "tii agano langu"

Hili ndilo agano langu

"Hili ni hitaji la agano langu" au "Hii ni sehemu ya agano langu". Sentensi hii inatambulisha sehemu ya agano ambayo Abramu ilimpasa afanye.

Kila mwanaume wa kwenu lazima atahiriwe

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Unapaswa kutahiri kila mwanamume miongoni mwako"

Kila mwanaume

Hii ina maana ya wanadamu wa kiume

Lazima mtatahiriwa katika nyama ya govi la ngozi ya mbele

Baadhi ya jamii inaweza kutumia lugha nyepesi zaidi kama "Unatakiwa kutairiwa." Iwapo tafsiri yako ya "fanya tohara" inajumlisha neno la govi la ngozi ya mbele, hauhitaji kurudia.Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Unatakiwa kuwatahiri wanamume wote miongoni mwenu"

ishara ya agano

"ishara inayoonyesha ya kwamba agano lipo"

ishara

Maana zaweza kuwa 1) "ishara" au 2) "ishara". Maana ya kwanza inaonyesha kulikuwa na ishara moja, na maana ya pili inaonyesha kulikuwa na ishara zaidi ya moja. Hapa neno "ishara" ina maana ya ukumbusho kuhusu jambo ambalo Mungu aliahidi.

Genesis 17:12

Taarifaya Jumla

Mungu anaendelea kuzungumza na Abrahamu.

Kila mwanaume

"Hii ina maana ya wanadamu wa kiume"

katika vizazi ya watu wenu

"katika kila kizazi"

yeye ambaye amenunuliwa kwa fedha

Hii ina maana ya watumwa. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "mwanamume yeyote utakayemnunua"

agano langu litakuwa katika mwili wenu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "utaweka alama ya agano langu juu ya mwili wako"

kuwa agano la milele

"kama agano la kudumu". Kwa sababu iliwekwa juu ya mwili, hakuna aliyeweza kuifuta.

Mwanaume yeyote asiye tahiriwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda, na unaweza kuacha maneno ambayo yanaweza kuleta maana mbaya katika lugha yako. "mwanamume ambaye haujamtahiri"

Mwanaume yeyote asiye tahiriwa ... govi la ngozi yake ya mbele atatengwa na watu wake

Maana zaweza kuwa 1) "nitamtenga mwanamume yeyote asiyetahiriwa ... govi la mbele kutoka kwa watu wake" au 2)"Ninataka umtenge mwanamume yeyote asiyetahiriwa ... govi la mbele kutoka kwa watu wake"

atatengwa na watu wake

Maana zaweza kuwa 1) "aliuawa" au 2) "kufukuzwa kutoka kwenye jamii".

Amevunja agano langu

"Hajatii amri za agano langu." Hii ni sababu itakayomfanya atengwe kutoka kwa watu wake.

Genesis 17:15

kwa habari ya Sarai

Maneno "kwa habari ya" zinatambulisha mtu anayefuata ambaye Mungu anamzungumzia.

nitakupatia mtoto wa kiume kwake

"Nitamfanya azae mtoto kupitia kwake"

atakuwa mama wa mataifa

"atakuwa mama wa mataifa mengi" au "uzao wake watakuwa mataifa"

Wafalme wa watu wa mataifa watapatikana kutokana na yeye

"Wafalme wa watu watatokana kwake" au "Baadhi ya uzao wake watakuwa wafalme wa watu"

Genesis 17:17

akasema moyoni mwake

"akawaza mwenyewe" au "akasema mwenyewe kimya kimya"

Je yawezekana mtoto azaliwe kwa mwanaume ambaye ana umri wa miaka mia moja?

Abrahamu alitumia swali hili la balagha kwa sababu hakuamini ya kuwa hili lingeweza kutokea. "Hakika mwanamume mwenye umri wa miaka mia moja hawezi kuwa baba wa mtoto!"

Je Sara, ambaye ana umri wa miaka tisini anaweza kuzaa mwana?

Tena Abrahamu alitumia swali la balagha kwa sababu hakuamini ya kuwa hili lingeweza kutokea. msemo "ambaye ana umri wa miaka tisini" unasema kwa nini Abrahamu hakuamini ya kwamba Sarai hataweza kuzaa mtoto. "Sarai ana umri wa miaka tisini. Hakika hawezi kuzaa mtoto wa kiume!"

Lau Ishmaeli angeweza kuishi kabla yako!

"Tafadhali muache Ishmaeli arithi agano ulilofanya pamoja na mimi" au "Huenda Ishmaeli anaweza kupokea baraka ya agano lako" Abrahamu alipendekeza jambo ambalo aliamini lingeweza kutokea"

Genesis 17:19

Hapana, Sarai mkeo atakuzalia

Mungu alisema hili kusahisha imani ya Abrahamu juu ya Sarai kupata mtoto.

utamwita jina lake

Neno "utamwita" linamlenga Abrahamu.

Na kwa habari ya Ishmaeli

Maneno "na kwa habari" yanaonyesha ya kwamba Mungu anabadilisha maongezi kuhusu mtoto ambaye angezaliwa na kumuongelea Ishmaeli.

Tazama

"Angalia" au "Sikiliza" au "Sikiliza kwa makini kwa kile nachotaka kukuambia"

nitamfanya kuwa na uzao

Hii ni lahaja inayokuwa na maana ya "nitamsababisha awe na watoto wengi"

na kumzidisha maradufu

"na nitamsababisha awe na uzao mwingi"

viongozi wa makabila

"machifu" au "watawala". Hawa viongozi sio wana kumi na mbili na wajukuu wa Yakobo ambao wataongoza makabila kumi na mbili ya Israeli.

Lakini agano langu nitalifanya imara na Isaka

Mungu anarudi kuongelea juu ya agano lako na Abrahamu na kusisitiza ya kwamba atatimiza ahadi yake na Isaka, na sio Ishmaeli.

Genesis 17:22

Alipo kuwa amemaliza kuzungumza naye

"Mungu alipomaliza kuzungumza na Abrahamu"

Mungu akaondoka kwa Abraham

"Mungu akamuacha Abrahamu"

kila mwanaume miongoni mwa watu wa nyumba ya Abraham

"kila binadamu wa kiume katika nyumba ya Abrahamu" au "kila mtu wa kiume katika nyumba ya Abrahamu". Ina maana ya wanadamu wa kiume wa umri wote: watoto wachanga, wavulana na wanamume.

Genesis 17:24

ni pamoja na wale waliozaliwa katika nyumba ile na wale walionunuliwa kwa fedha kutoka kwa mgeni

"Hii inajumlisha wale waliozaliwa katika nyumba yake na wale walionunuliwa kutoka kwa wageni"

wale walionunuliwa kwa fedha kutoka kwa mgeni

Hii ina maana ya watumishi au watumwa

wale walionunuliwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "wale ambao amekwisha wanunua"

Genesis 18

Genesis 18:1

Mamre

Hili lilikuwa jina la mwanamume aliyemiliki mialoni.

mlangoni pa hema

"katika uwazi wa hema" au "katika kuingilia kwa hema"

joto la mchana

"wakati wa jua kali la mchana"

Akatazama juu na, tazama, akaona wanaume watatu wamesimama.

"Alitazama juu na kuona, tazama, wanamume watatu walikuwa wamesimama"

tazama

"ghafla". Neno "tazama" hapa linatuonyesha kitakachofuata ni cha kushangaza kwa Abrahamu.

mbele yake

"karibu" au "pale". Walikuwa karibu na yeye, lakini umbali wa kutosha kwa yeye kuwakimbilia.

kuinama

Hii ina maana kuinama chini na kuonyesha unyenyekevu na heshima kwa mtu.

Genesis 18:3

Bwana

Hili ni jina la heshima. Maana zaweza kuwa 1) Abrahamu alijua ya kuwa mmoja wa wanamume hawa alikuwa Mungu au 2) Abrahamu alijua ya kwamba wanamume hawa walikuja kwa niaba ya Mungu.

machoni pako

Abrahamu anazungumza na mmoja wa wanamume.

usinipite

"tafadhali msiendelee kupita"

mtumishi wako

"mimi". Abrahamu ana maanisha yeye mwenyewe katika njia hii kuonyesha heshima kwa mgeni wake.

Naomba maji kidogo yaletwe

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Niruhusu nikuletee maji" au "Mtumishi wangu atakuletea maji"

maji kidogo ... chakula kidogo

"maji kidogo ... chakula kidogo." Kusema "kidogo" ilikuwa lugha ya upole ya kuonyesha ukarimu. Abrahamu angewapatia maji na chakula cha kutosha zaidi.

mnawe miguu yenu

Utamaduni huu uliwasaidia wasafiri waliochoka kujiburudisha baada ya kutembea umbali mrefu.

wenu ... mji...

Abrahamu anazungumza na wanamume wote watatu, kwa hiyo "wenu" na "mji..." ni katika hali ya wingi.

Genesis 18:6

vipimo vitatu

kama lita 22

mkate

Mkate huu yawezekana ulikuwa umepikwa haraka katika jiko la moto. Inawezekana ulikuwa tambarare au duara kama mikate midogo midogo ya duara.

kwa haraka

"mtumishi aliharakisha"

akaiandaa

"kuukata na kuubanika"

siagi

Hii ina maana ya sehemu ngumu ya maziwa yaliogandishwa. Inawezekana ilikuwa mtindi au jibini.

ndama aliye kwisha andaliwa

"ndama aliyebanikwa"

mbele yao

"mbele ya wageni watatu"

Genesis 18:9

Wakamwambia

"Kisha wakamwambia Abrahamu"

akasema, "Hakika nitarejea kwako

Neno "akasema" lina maana ya mwanamume ambaye Abrahamu alimwita "Bwana" katika 18:3.

majira ya machipuko

"pale ambapo majira kama haya yatakapowadia mwaka kesho" au "muda kama huu mwaka kesho"

na tazama

Neno "tazama" hapa linatutahadharisha kuwa makini kwa taarifa ya kushangaza inayofuata.

mlangoni pa hema

"katika uwazi wa hema" au "katika kiingilio cha hema"

Genesis 18:11

baada ya kuwa nimechakaa na bwana wangu ni mzee, je ni tapata furaha hii?

nimechakaa na bwana wangu ni mzee, je nitapata furaha hii ya kupata mtoto? Sarai alitumia swali hili la balagha kwa sababu hakuamini angeweza kupata mtoto. "Siamini ya kuwa nitapitia furaha ya kupata mtoto. Bwana wangu ni mzee sana"

bwana wangu ni mzee

Hii ina maana ya "kwa kuwa mume wangu ni mzee pia".

bwana wangu

Hili ni jina la heshima ambalo Sarai alimpa mumewe Abrahamu.

Genesis 18:13

Kwa nini Sara amecheka na kusema, Je ni kweli nitazaa mtoto, nikiwa mzee'?

Mungu alitumia swali la balagha kuonyesha ya kwamba alifahamu alichokuwa akikifikiria Sarai na ya kwamba hakufurahishwa nacho. Anarudia swali la balagha la Sarai (18:11) kutumia maneno tofauti. "Sarai hakuwa sahihi kucheka na kusema, "Sitazaa mtoto kwa sababu mimi ni mzee sana!"

Je kuna jambo lolote gumu sana kwa Yahwe?

"Je kuna jambo lolote ambalo Yahwe hawezi kufanya?" Yahwe anazungumzia juu yake mwenyewe kana kwamba anazungumzia mtu mwingine kumkumbusha Abrahamu ya kwamba yeye, Yahwe, ni mkuu na anaweza lolote. "Hakuna jambo ambalo mimi, Yahwe, siwezi kufanya!"

katika wakati nilioweka mimi majira ya machipuko

"Katikamuda huo niliouweka, ambao ni wakati wa machipuko"

Kisha Sarai akakataa na kusema

"Kisha Sarai aliukana kwa kusema"

akajibu

"Yahwe alijibu"

hapana ulicheka

"Ndio, ulicheka." Hii ina maana ya "Hapana, hiyo sio kweli; kweli umecheka."

Genesis 18:16

kuwaaga

"kuwaaga kwenda njia yao" au "kusema 'Kwaheri' kwao". Ilikuwa ni jambo la upole kuwasindikiza wageni umbali fulani wakati wanapoondoka.

Je ni mfiche Abraham kile ninacho kusudia kufanya ...yeye?

Mungu alitumia swali hili la balagha kusema ya kwamba alikuwa akizungumza na Abrahamu kuhusu jambo muhimu sana na kwamba ilimpasa yeye kufanya hivyo. "Sipaswi na sitamficha Abrahamu kile ninachotaka kufanya .... yeye." au "Ninatakiwa na nitamwambia Abrahamu kile ninachotaka kufanya ... yeye"

Je ni ... kufanya, kwa kuwa ... yeye?

"Sitakiwi ... kufanya. Hii ni kwa sababu .. yeye"

katika yeye mataifa yote ya dunia watabarikiwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Nitawabariki mataifa yote ya duniani kupitia Abrahamu.

katika yeye watabarikiwa

"watabarikiwa kwa sababu ya Abrahamu" au "watabarikiwa kwa sababu nimembariki Abrahamu".

ili awaelekeze

"ya kwamba atawaongoza" au "ili kwamba awaamuru"

waishike njia ya Yahwe ... Yahwe ampatie ... aliyo yasema

Yahwe anazungumza juu yake mwenyewe kana kwamba alikuwa mtu mwingine. "kutii kile ambacho mimi, Yahwe nahitaji....mimi, Yahwe, nitaleta ... nimesema"

waishike njia ya Yahwe

"kutii amri za Yahwe"

watende utakatifu na haki

"kwa kufanya utakatifu na haki" Hii inaelezea namna ya kushikilia njia ya Yahwe.

ili kwamba Yahwe ampatie Abraham yale aliyo yasema kwake

"ili kwamba Yahwe aweze kumbariki Abrahamu kama alivyosema angefanya" Hii ina maana ya ahadi ya agano ya kumbariki Abrahamu na kumfanya kuwa taifa kubwa.

Genesis 18:20

kilio cha Sodoma na Gomora ni kikuu

Hii inaweza kuelezwa kwa maneno mengine ili maana halisi ya "kilio" linaloelezwa kama kitenzi cha "kushtaki". "watu wengi sana walikuwa wakishtaki watu wa Sodoma na Gomora kufanya uovu mwingi"

dhambi yao ni kubwa

"wamefanya dhambi sana"

sasa nitashuka pale

"Nitashuka pale sasa hadi Sodoma na Gomora"

nitashuka pale na kuona

"nitashuka pale kujua" au "nitashuka pale kuamua"

kuona kilio ... kilicho nifikia

Yahwe anazungumzia kana kwamba alijua kuhusu jambo hili kwa sababu alisikia kilio na mashtaka yakija kutoka kwa watu waliokuwa wameteseka. Hii inaweza kuwekwa kwa maneno mengine ili kitenzi cha "kilio" kiweze kuelezwa kama kitenzi cha "kushtaki". "waovu kama wale wanaowashtaki wanasema kuwa wako vile"

ikiwa kweli

"kama sio waovu kama kilio kinavyoashiria"

Genesis 18:22

wakageuka toka pale

"aliondoka kutoka katika hema la Abrahamu"

Abrahamu akabaki amesimama mbele ya Yahwe

"Abrahamu na Yahwe walibaki pamoja"

alikaribia

"alimkaribia Yahwe" au "alisogea karibu na Yahwe"

utawafutilia mbali

Abrahamu anazungumzia kuwaangamiza watu kana kwamba alikuwa akifagia takataka kwa ufagio. "kuangamiza"

watakatifu pamoja na waovu

"watu watakatifu na watu waovu"

Genesis 18:24

Taarifa ya Jumla:

Abrahamu anaendelea kuzungumza na Yahwe

Huenda wakawepo

"Chukulia wakawepo"

Je utawakatilia mbali na usiuache mji kwa ajili ya hao watakatifu hamsini walioko hapo?

Abrahamu alikuwa na tumaini ya kwamba Yahwe angesema, "Sitaikatalia mbali". "Nadhani hautaikatalia mbali. Badala yake, utaiacha kuiharibu sehemu kwa sababu ya watakatifu hamsini ambao wapo pale"

utawakatilia mbali

"kuingamiza". Abrahamu anazungumzia kuwaangamiza watu kana kwamba alifagia uchafu na ufagio. "kuangamiza watu waliokuwa wakiishi pale"

na usiuache mji kwa ajili ya hao watakatifu hamsini walioko hapo?

Abrahamu alikuwa akitumaini ya kwamba Mungu angesema, "Nitaacha kuangamiza sehemu kwa niaba ya watu watakatifu hamsini walioishi pale"

usiuache mji

"ruhusu watu waishi"

kwa ajili ya hao

"kwa sababu ya"

Hasha usifanye hivyo

"Sitapenda ufanye jambo kama hilo" au "Haupaswi kutaka kufanya jambo kama hilo"

hivyo, kuwauwa

"jambo kama hili kama kuwaua" au "jambo kama hilo, yaani, kuwaua"

watakatifu watendewe sawa na waovu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "unatakiwa kuwatendea watakatifu sawa sawa na waovu"

Je Mhukumu wa ulimwengu wote hatatenda haki?

Abrahamu alitumia swali hili la balagha kusema kile alichotarajia Mungu kukifanya. "Mhukumu wa ulimwengu wote hakika atafanya kilicho haki" au "Kwa kuwa wewe ni Mhukumu wa ulimwengu wote, hakika utafanya lililo sahihi!"

Mhukumu

Mungu anasemwa kama mhukumu kwa sababu yeye ni mhukumu aliye kamilika ambaye hufanya maamuzi ya mwisho kuhusu mema na mabaya.

Genesis 18:27

Tazama

Msemo wa "tazama" hapa unavuta nadhari juu ya taarifa ya kushangaza inayofuata.

Nimeshika kusema

"Niwie radhi kwa kuwa wazi na kuzungumza na wewe" au "Samahani kwa kudiriki kuzungumza"

kwa Bwana wangu

Abrahamu anaonyesha heshima kwa Yahwe kwa kuzungumza na Yahwe kana kwamba alikuwa akizungumza na mtu mwingine. "kwako wewe, Bwana wangu"

mavumbi na majivu

Sitiari hii inamuelezea Abrahamu kama binadamu, ambaye atakufa na mwili wake kugeuka kuwa vumbi na majivu. "ni binadamu pekee" au "kama vile vumbi na majivu yasivyokuwa na umuhimu"

watano pungufu katika idadi ya hao watakatifu hamsini

"watu arobaini na tano tu watakatifu"

kwa upungufu wa hao watano

"iwapo kuna watu watano pungufu watakatifu"

Sitaangamiza

"Sitaangamiza Sodoma"

Genesis 18:29

Akaongea naye

"Abrahamu akazungumza na Yahwe"

ikiwa arobaini watapatikana pale

Hii ina maana ya "ikiwa ukapata watu watakatifu arobaini Sodoma na Gomora"

Akajibu

"Yahwe akajibu"

Sitafanya kwa ajili ya hao arobaini

"Sitaangamiza miji iwapo nitakuta watu watakatifu arobaini pale"

thelathini

"watu thelathini watakatifu" au "watu thelathini wazuri"

Tazama

Msemo wa "tazama" hapa unavuta nadhari juu ya taarifa ya kushangaza inayofuata.

Nimeshika kusema

"Niwie radhi kwa kuwa wazi na kuzungumza na wewe" au "Samahani kwa kudiriki kuzungumza"

ishirini

"watu ishirini watakatifu" au "watu ishirini wazuri"

Genesis 18:32

Huenda kumi wakaonekana kule

"Huenda utakuta watu kumi watakatifu pale"

kumi

"watu kumi watakatifu" au " watu kumi wazuri"

Kisha akasema

"Na Yahwe akajibu"

kwa ajili ya hao kumi

"ikiwa nikipata watu kumi watakatifu pale"

Yahwe akaendelea na njia yake

"Yahwe aliondoka" au "Yahwe alienda"

Genesis 19

Genesis 19:1

Malaika wawili

Mwanzo 18 unasema ya kwamba wanamume wawili waliondoka kwenda Sodoma. Hapa tunajifunza ya kwamba ni kweli walikuwa malaika.

langoni mwa Sodoma

"malango wa mji wa Sodoma." Mji ulikuwa na kuta ukiuzunguka, na watu iliwabidi kupitia malango ili kuingia. Hii ilikuwa sehemu muhimu sana katika mji. Watu muhimu mara kwa mara walitumia muda wao pale.

akainama uso wake chini ardhini

Aliweka goti lake juu ya ardhi na kisha kugusa ardhi kwa kipaji cha uso wake na pua.

Bwana zangu

Huu ulikuwa usemi wa heshima Lutu alitumia kwa malaika.

nawasihi mgeuke mwende kwenye nyumba ya mtumishi wenu

"Tafadhali njooni na mkae ndani ya nyumba ya mtumishi wenu"

nyumba ya mtumishi wenu

Lutu anajitambulisha kama mtumishi ili kuonyesha heshima kwao.

muoshe miguu yenu

Watu walipenda kuosha miguu yao baada ya kusafiri.

muamke asubuhi

"muamke mapema"

usiku tutalala

Malaika wawili waliposema hivi, walikuwa wakimaanisha wao wenyewe, na sio Lutu. Wao wawili walipanga kukaa usiku pale mjini.

mjini

Hili ni eneo la wazi, lililo nje katika mji.

wakaondoka pamoja nae

"waligeuka na kuondoka pamoja naye"

Genesis 19:4

kabla hawaja lala

"kabla watu ndani mwa nyumba ya Lutu walipolala usingizi"

wanaume wa mji, wa Sodoma

"wanamume wa mji, yaani, wanamume wa Sodoma" au "wanamume wa mji wa Sodoma"

nyumba

"nyumba ya Lutu"

vijana kwa wazee

"kutoka kwa vijana hadi wazee". Hii ina maana "wanamume wa umri wote" na ina maana ya wanamume wa Sodoma ambao walikuwa wakizunguka nyumba ya Lutu.

walioingia kwako

"waliongia ndani ya nyumba"

kulala nao

"kushiriki tendo la ngono pamoja nao". Lugha yako yaweza kuwa na namna ya upole zaidi ya kusema hivi. "kuwajua karibu zaidi"

Genesis 19:6

nyuma yake

"nyuma yake" au "baada ya kuingia ndani"

Nawasihi, ndugu zangu

"nawaomba, ndugu zangu"

ndugu zangu

Lutu alizungumza kwa njia ya kirafiki kwa wanamume wa mji akitarajia wangemsikiliza. "rafiki zangu"

msitende uovu

"msifanye jambo la uovu hivi" au "msifanye jambo la uovu kama hili"

Tazama

"Sikiliza kwa makini" au"Angalia hapa"

hawajawahi kulala na

"hawajashiriki tendo la ngono na" Lugha yako inaweza kuwa na njia ya upole ya kusema hili. "hawajawajua"

lolote muonalo kuwa jema machoni penu

"lolote mnalotamani" au "lolote mnalofikiria ni sahihi"

chini ya kivuli cha dari yangu

Wanamume wawili walikuwa wageni katika nyumba ya Lutu, kwa hiyo alihitaji kuwalinda. Neno "dari" ni maana nyingine ya kusema nyumba na sitiari kwa Lutu kuwalinda. "ndani ya nyumba yangu, na Mungu anatarajia mimi niwalinde"

Genesis 19:9

Simama nyuma!

"Simama pembeni!" au "Toka katika njia yetu!"

huyu alikuja kukaa hapa kama mgeni

"Huyu hapa alikua hapa kama mtu wa nje" au "Huyu mgeni alikuja kuishi hapa"

huyu

"Lutu". Wanamume wanazungumza wao kwa wao. Kama hii haitakuwa wazi katika lugha yako, unaweza kuwafanya wanamume wazungumze na Lutu hapa.

na sasa amekuwa mwamuzi wetu

"na sasa anadhani ana mamlaka ya kutuambia kipi ni sahihi na kipi sio sahihi" au "lakini hatutamruhusu atuzuie kufanya kile tunachotaka kufanya"

na sasa ame...

"na ingawa hana sababu nzuri, amekuwa"

Sasa tuta...

"Kwa sababu unatuambia ya kwamba tunafanya uovu, tuta.."

tutakushugulilia vibaya wewe kuliko wao

Wanamume walikasirika kwa Lutu kusema, "Msitende uovu hivi" (19:6) kwa hiyo wanamtishia kutenda uovu zaidi ya vile Lutu alivyohofia mara ya kwanza. "tutakushughulikia uovu zaidi na wewe zaidi ya wao"

Wakamsonga sana huyo mtu, huyo Lutu, na wakakaribia kuvunja mlango

Maana zaweza kuwa 1) "walizidi kuja karibu na mwanamume, kwa Lutu, hadi wakawa karibu sana kuweza kuvunja mlango" au 2) walimsukuma Lutu kwa mwili dhidi ya ukuta au mlango wa nyumba na walikuwa wakitaka kuvunja mlango.

huyo mtu ... Lutu

Hizi ni njia mbili zinazomfafanua Lutu.

Genesis 19:10

Lakini wale wanaume

"Lakini wageni wawili wa Lutu" au "Lakini malaika wawili"

wanaume wakamkamata Lutu na kumweka ndani na wakafunga

Lugha yako inaweza kuongezea ya kwamba wanamume walifungua mlango kwanza. "wanamume walifungua mlango vya kutosha mpaka kunyosha mikono yao na kuvuta ... na kisha wakafunga"

wageni wa Lutu wakawapiga kwa upofu wale wanaume

Msemo "wakawapiga kwa upofu" ni sitiari; wageni hawakuwapiga kwa mwili wanamume. "Wageni wa Lutu waliwapofusha wanamume" au "waliondoa uwezo wao wa kuona"

vijana na wazee kwa pamoja

"wanamume wa umri wote". Hii lugha unasisitiza ya kwamba wageni walipofusha wanamume wote. Hii inaweza kumaanisha uwakilishi wa kijamii kuliko umri. "vijana na wazee kwa pamoja"

Genesis 19:12

Basi wale watu wakamwambia

"Kisha wale wanamume wawili wakasema" au "Kisha malaika wawili wakasema"

Je una mtu mwingine yeyote hapa?

"Je una mtu mwingine wa familia yako ndani ya mji?" au "Je una mtu mwingine wa familia katika eneo hili?"

yeyote mwingine katika huu mji

"mtu mwingine katika familia yako anayeishi katika mji huu"

tunakaribia kuiangamiza

Neno "tunakaribia" hapa linajitegemea. Ni malaika wawili pekee wangeenda kuangamiza mji; Lutu hakuwa anaenda kuangamiza mji. Iwapo lugha yako ina namna ya kutenganisha "tunakaribia" basi itumike hapa.

mashitaka dhidi yake mbele ya Yahwe yamezidi

Hii inaweza kusemwa kwa namna nyingine ili kwamba nomino ya "mashtaka" inaelezwa kama kitenzi. "kwa hiyo watuwengi walikuwa wakimwambia Yahwe ya kwamba watu wa mji wanafanya mambo ya uovu"

Genesis 19:14

Lutu akatoka

"Kwa hiyo Lutu aliondoka nyumbani"

wakwe zake, wanaume ambao walikuwa wamewaposa binti zake

wakwe zake, wanaume ambao walikuwa wamewaposa binti zake Msemo wa "wanaume ambao walikuwa wamewaposa binti zake" unafafanua maana ya "mkwe" hapa. "wanamume waliokuwa wakielekea kuwaoa binti zake" au "wachumba wa binti zake"

Alfajiri

"Kabla jua halijachomoza"

ondoka

"Ondoka sasa"

usipotelee katika adhabu ya mji huu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ili Yahwe asikuangamize pia atakapowaadhibu watu wa mji huu"

usipotelee katika adhabu

Mungu kuangamiza watu wa mji unazungumzwa kana kwamba mtu anafagia vumbi.

ya mji

Hapa "mji" una maana ya watu.

Genesis 19:16

Lakini akakawia-kawia

"Lakini Lutu alisita" au "Lakini Lutu hakuanza kuondoka"

Kwa hiyo watu wale wakamshika

"kwa hiyo wanamume wawili walimkamata" au "Kwa hiyo malaika walimkamata"

alimhurumia

"akawa na huruma kwa Lutu". Yahwe anaelezwa kama kuwa na "huruma" kwa sababu alikuwa akitunza uhai wa Lutu na familia yake badala ya kuwaangamiza alipoangamiza watu wa Sodoma kwa maovu waliofanya.

Walipowatoa nje

"Wanamume wawili walipowatoa familia ya Lutu nje"

jiponye nafsi yako!

Hii ilikuwa namna ya kuwaambia wakimbie ili wasife. "Kimbia na uokoe maisha yenu!"

usitazame nyuma

Msemo "katika mji" unaeleweka. "Usitazame nyuma katika mji" au "Usitazame nyuma katika Sodoma"

kwenye hili bonde

Hii ina maana bonde la Mto Yordani. Hii ina maana ya jumla ya eneo la Mto Yordani.

usije ukatoweshwa mbali

Inaeleweka ya kwamba watatoweshwa pamoja na watu wa mji. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "la sivyo Mungu atawaangamiza pamoja na watu wa mji"

ukatoweshwa mbali

Mungu kuwaangamiza watu wa mji inazungumziwa kana kwamba mtu anafagia vumbi.

Genesis 19:18

Mtumishi wenu amepata kibali machoni pako

Kupendezwa na mtu inazungumziwa kana kwamba "fadhila" ni kitu kinachoweza kupatikana. Pia, "machoni" ni lugha nyingine inayowakilisha mawazo au fikra za mtu. "Umependezwa na mimi"

Mtumishi wenu ame...

Lutu alikuwa akionyesha heshima kwa kumaanisha mwenyewe kama "mtumishi wako". "Mimi, mtumishi wako, nime..."

umenionesha wema ulio mkuu kwa kuokoa maisha yangu

Kitenzi cha "wema" kinaweza kuelezwa kama "wema". "Umekuwa mwema sana kwangu kwa kuokoa maisha yangu"

sitaweza kutorokea milimani, kwa sababu mabaya yataniwahi na nitakufa

Kutoweza kufika umbali wa kutosha mwa Sodoma pale ambapo Mungu anaangamiza mji unazungumziwa kana kwamba "uhalifu" ni mtu ambaye atamfukuza na kumfikia Lutu. "Familia yangu na mimi hakika tutakufa Mungu atakapoangamiza watu wa Sodoma, kwa sababu milima ipo mbali sana na sisi kufika kule salama"

maisha yangu ... sitaweza kutorokea ... yataniwahi na nitakufa

Inaonyesha ya kwamba familia ya Lutu itakufa pamoja naye. "maisha yetu ... hatuwezi kutoroka ... yataniwahi, na tutakufa"

niacheni nikimbilie pale ( Je Siyo mdogo ule?), na maisha yangu yataokolewa

Lutu alitumia swali hili la balagha kuwafanya malaika kutambua ya kwamba ule mji ni mdogo kweli. "acha nitoroke kule. Unaona jinsi gani ni mdogo. Ukituruhusu kufika pale tutaishi"

niacheni nikimbilie pale

Ombi kamili la Lutu linaweza kuwekwa wazi. "badala ya kuangamiza mji ule, niruhusu nitoroke pale"

maisha yangu yataokolewa

Inaonyesha ya kwamba maisha ya familia ya Lutu yataokolewa pamoja naye. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ili kwamba tuweze kuishi" au "ili kwamba tuweze okoka"

Genesis 19:21

nimekubali ombi hili pia

"nitafanya kile ulichokiomba"

sitafanya chochote

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "sitaangamiza miji mingine"

Soari

Watafsiri wanaweza kuongeza maandishi yanayosema "Jina la Soari linafanana na neno la Kiebrania lenye maana ya "ndogo". Lutu aliuita mji huu "mdogo" katika Mwanzo 19:20.

Genesis 19:23

Jua lilikuwa limekwisha chomoza juu ya nchi

"Jua limechomoza juu ya nchi". msemo wa "juu ya nchi" unaweza kuachwa wazi.

Lutu alipofika Soari

Inaonyesha ya kwamba familia ya Lutu ilikuwa pamoja naye. "Lutu na familia yake walipofika Soari"

Yahwe akanyesha juu ya Sodoma na Gomora kiberiti na moto toka kwa Yahwe mbinguni

Msemo wa "kutoka kwa Yahwe" una maana ya nguvu ya Mungu kusababisha kiberiti na moto kuanguka juu ya mji. Yahwe alisababisha kiberiti na moto kuanguka kutoka mbinguni juu ya Sodoma na Gomora"

kiberiti na moto

Maneno haya yanatumika pamoja kuelezea umbo moja. "kiberiti kiwakacho" au "mvua kali"

miji ile

Kimsingi hii ina maana ya Sodoma na Gomora, lakini pia miji mingine mitatu.

vilivyomo katika miji

"watu waliokuwa wakiishi katika miji ile"

Genesis 19:26

akawa nguzo ya chumvi

"akawa kama sanamu ya chumvi" au "mwili wake ukawa kama jiwe refu la chumvi". Kwa sababu hakutii malaika aliyemwambia asitazame nyuma ya mji, Mungu alimfanya awe kama sanamu iliyotengenezwa na jiwe la chumvi.

tazama

Msemo wa "tazama" hapa unavuta nadhari juu ya taarifa ya kushangaza inayofuata.

kama moshi wa tanuru

Hii inaonyesha ya kwamba ulikuwa ni moshi mkubwa sana. "kama moshi utokao katika moto mkubwa sana"

Genesis 19:29

Taarifa ya Jumla:

Mstari wa 29 ni ufupi wa sura hii.

Mungu akamkumbuka Abrahamu

Hii inasema kwa nini Mungu alimuokoa Lutu. "kukumbuka" ni namna ya kusema "alimkumbuka". Hii haimaanishi Mungu alisahau juu ya Abrahamu. Ina maana alimfikiria Abrahamu na kuwa na huruma juu yake. "Mungu alimfikiria Abrahamu na kuwa na huruma juu yake"

katika maangamizi

"kutoka kwa maangamizi" au "kutoka kwa hatari"

Genesis 19:30

Lutu akapanda juu kutoka Soari na kwenda kuishi katika milima

Msemo "akapanda juu" unatumiwa kwa sababu Lutu alienda sehemu ya juu mlimani.

Genesis 19:31

Yule wa kwanza

"Binti wa kwanza wa Lutu" au "Binti mkubwa"

yule mdogo

"Binti mdogo" au "mdogo wake"

kulingana na desturi ya dunia yote

Hapa "dunia" ina maana ya watu. "kama watu sehemu zote hufanya"

kunywa mvinyo

Hii inaweza kuelezwa kwa uwazi ya kwamba lengo lao lilikuwa kumfanya alewe. "kunywa mvinyo hadi alewe" au "alewe kwa mvinyo".

ili kwamba tuendeleze uzao wa baba yetu

Hii inazungumzia kuhusu kumpatia Lutu uzao kana kwamba familia yake ilikuwa na mtiririko mrefu. "ili kwamba tuweze kuzaa watoto ambao watakuwa uzao wa baba yetu"

hakujua ni wakati gani alikuja kulala, wala wakati alipo amka

"hakujua chochote kuhusu hili" au "hakujua ya kwamba alilala pamoja naye"

Genesis 19:34

Na tumnyweshe mvinyo ... wala wakati alipoamka

Hii inaweza kuelezwa kwa uwazi ya kwamba lengo lao lilikuwa kumfanya alewe. "kunywa mvinyo hadi alewe" au "alewe kwa mvinyo".

tumnyweshe mvinyo

Hii inaweza kuelezwa kwa uwazi ya kwamba lengo lao lilikuwa kumfanya alewe. "kunywa mvinyo hadi alewe" au "alewe kwa mvinyo".

Ili kwamba tuendeleze uzao wa baba yetu

Hii inazungumzia kuhusu kumpatia Lutu uzao kana kwamba familia yake ilikuwa na mtiririko mrefu. "ili kwamba tuweze kuzaa watoto ambao watakuwa uzao wa baba yetu"

hakujua ni wakati gani alilala, wala wakati alipoamka

"hakujua chochote kuhusu hili" au "hakujua ya kwamba alilala pamoja naye"

Genesis 19:36

wakapata mimba kwa baba yao

"wakawa mimba kupitia baba yao" au "wakapatawatoto kwa baba yao"

Akawa

"Yeye ndiye"

wamoabu hata leo

"Wamoabu ambao wanaishi sasa"

hata leo

Neno "leo" lina maana ya kipindi ambapo mwandishi wa Mwanzo alipokuwa hai. Mwandishi alizaliwa na kuandika haya miaka mingi baada ya familia ya Lutu kuishi na kufa.

Benami

Hili ni jina la mwanamume.

watu wa Waamoni

"uzao wa Amoni" au "Watu wa Amoni"

Genesis 20

Genesis 20:1

Shuri

Hili ni eneo la jangwa upande wa mashariki wa mpaka wa Misri.

akatuma watu wake kumchukua Sara

"aliwafanya wanamume wake kumfuata Sara na kumleta kwake"

Mungu akamtokea Abimeleki

"Mungu akamtokea Abimeleki"

Tazama

Hapa neno "tazama" linaongeza msisitizo kwa kile kifuatacho. "Nisikilize"

wewe ni mfu

Hii ni njia ya nguvu ya kusema mfalme atakufa. "hakika utakufa hivi karibuni" au "Nitakuua"

mke wa mtu

"mwanamke aliyeolewa"

Genesis 20:4

Basi ... hajamkaribia

Neno hili linatumika hapa kuweka alama ya kubadilisha kutoka kwenye simulizi kwenda kwa taarifa kuhusu Abimeleki.

Abimeleki alikuwa bado hajamkaribia

Hii ni njia ya upole ya kusema hakufanya ngono pamoja naye. "Abimeleki hakulala na Sara" au "Abimeleki hakumgusa Sara"

hata taifa lenye haki

Hapa "taifa" lina maana ya watu. Abimeleki ana wasiwasi ya kwamba Mungu atawaadhibu sio yeye tu, lakini watu wake pia. "hata watu wasio kuwa na hatia"

Je si yeye mwenyewe aliye niambia, 'Sara ni dada yangu?' Hata Sara mwenyewe alisema, 'ni kaka yangu.'

Hii ina nukuu ndani ya nukuu. Zinaweza kutajwa kwa nukuu isiyo dhahiri. "Je sio yeye mwenyewe aliyeniambia ya kwamba huyo ni dada yaek? Hata yeye mwenyewe alinimbia ya kwamba ni kaka yake"

Je si yeye mwenyewe aliye niambia, 'Sara ni dada yangu?

Abimeleki alitumia swali la balagha kumkumbusha Mungu juu ya jambo alilokuwa akilifahamu tayari. Hii inaweza kufanywa kuwa kauli. "Abrahamu mwenyewe aliniambia 'Huyu ni dada yangu'" au "Abrahamu alisema ya kwamba ni dada yake".

Je si yeye mwenyewe aliye niambia, ...Hata Sara mwenyewe

Maneno "yeye mwenyewe" na "Sara mwenyewe" yanatumika kuweka msisitizo kuleta nadhiri kwa Abrahamu na Sara na kuwalaumu kwa kilichotokea.

Nimefanya hili katika uadilifu wa moyo wangu na katika mikono isiyo na hatia.

Hapa "moyo" una maana ya mawazo yake au nia zake. Pia "mikono" hapa ina maana ya matendo yake. "Nimefanya hili kwa nia njema na matendo mema" au "Nimefanya hivi bila mawazo au matendo ya uovu"

Genesis 20:6

Mungu akasema naye

"Mungu akasema kwa Abimeleki"

umefanya hili katika uadilifu wa moyo wako

Hapa"moyo" una maana ya mawazo na nia zake. "ulifanya hivi kwa nia njema" au "ulifanya hivi bila kuwa na nia ya uovu"

umshike

Hii ni lugha ya upole kwa kufanya ngono na Sara. "kulala naye"

mke wa mtu

"Mke wa Abrahamu"

utaishi

"Nitakuruhusu uishi"

wote walio wa kwako

"nyie watu wote"

Genesis 20:8

Akawasimulia mambo haya yote

"Aliwaambia kila kitu ambacho Mungu alimwambia"

Umetufanyia jambo gani?

Abimeleki alitumia swali hili la balagha kumshtaki Abrahamu. "Umefanya jambo hili baya kwetu!" au "Tazama ulichokifanya kwetu!"

Umetufanyia

Neno "umetufanyia" hapa linajitegemea na halimhusu Abrahamu na Sara.

Ni kwa jinsi gani nimekutenda dhambi kwamba umeniletea ... dhambi?

Abimeleki alitumia swali hili la balagha kumkumbusha Abrahamu ya kwamba hakufanya dhambi dhidi ya Abrahamu. "Sijafanya jambo dhidi yako kusababisha wewe ulete ... dhambi."

kwamba umeniletea mimi na ufalme wangu dhambi hii kubwa

Kumsababishia mtu awe na hatia ya kutenda dhambi inazungumzwa kana kwamba "dhambi" ilikuwa jambo linaloweza kuwekwa juu ya mtu. "ya kwamba umetufanya mimi na ufalme wangu kuwa na hatia kwa dhambi hii mbaya"

ufalme wangu

Hapa "ufalme" ina maana ya watu. "juu ya watu wa ufalme wangu"

Umenifanyia mimi jambo ambalo halipaswi kufanywa

"Usingefanya jambo hili kwangu"

Genesis 20:10

Nini kilikushawishi wewe kutenda jambo hili?

"Nini kilisababisha ufanye hivi?" au "Kwa nini ulifanya hivi?" Kile ambacho Abrahamu alifanya kinaweza kuwekwa wazi. "Kwa nini uliniambia ya kwamba Sara ni dada yako?"

kwasababu nilifikiri hakika hakuna hofu ya Mungu katika sehemu hii, na kwamba wataniua kwa ajili ya mke wangu.

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kusemwa katika nukuu tofauti. "Kwa sababu nilidhani ya kwamba kwa kuwa hakuna mwenye hofu ya Mungu hapa, mtu anaweza kuniua ili amchukue mke wangu"

hakuna hofu ya Mungu katika sehemu hii

Hapa "sehemu" ina maana ya watu. "hakuna mtu hapa Gerari mwenye hofu ya Mungu"

hofu ya Mungu

Hii ina maana ya kumheshimu Mungu sana na kuonyesha heshima hiyo kwa kumtii.

Licha ya kwamba kweli ni dada yangu

"Pia, ni kweli ya kwamba Sara ni dada yangu" au "Pia, Sara ni dada yangu ki ukweli"

binti wa baba yangu, ingawa si binti wa mama yangu

"tuna baba mmoja, lakini mama tofauti"

Genesis 20:13

Taarifa ya Jumla:

Mstari wa 13 ni muendelezo wa jibu la Abrahamu kwa Abimeleki.

nyumba ya baba yangu

Hapa "nyumba" ina maana ya familia ya Abrahamu. "baba yangu na familia yangu yote" au "nyumba ya baba yangu"

nilimwambia mke wangu, kwa kila sehemu tutakayo kwenda, unioneshe uaminifu wako kama mke wangu: Kila mahali tutakapo kwenda, useme juu yangu kuwa, "Ni kaka yangu."'''

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kusemwa katika nukuu tofauti. "Nilisema kwa Sara ya kwamba nataka awe mwaminifu kwangu kwa kuwaambia watu kila mahali tuendapo ya kwamba mimi ni kaka yake"

Abimeleki akatwaa

"Abimeleki akaleta baadhi"

Genesis 20:15

Abimeleki akasema

"Abimeleki akasema kwa Abrahamu"

Tazama

Hapa na katika mstari wa 16 neno "tazama" linaongeza msisitizo kwa kile kifuatacho.

Nchi yangu i mbele yako

Hii ni njia ya kusema "ninaifanya nchi yangu yote iwe wazi kwako"

Kaa mahali utakapopendezewa

"ishi popote upendapo"

elfu

"1,000"

ni kwa ajili ya kufunika kosa lolote dhidi yako machoni pa wote walio pamoja na wewe

Kutoa fedha kuthibitisha kwa wengine ya kwamba Sara hana hatia inazungumzwa kana kwamba anaweka mfuniko juu ya kosa ili mwingine asilione. "Ninampatia hili kwake, ili kwamba wale ulionao wajue haujafanya kosa"

machoni

Hapa "macho" ina maana ya mawazo na fikra za mtu.

mbele ya kila mtu ambaye umemfanya kuwa na haki

Msemo huu wa "umemfanya kuwa na haki" unaweza kuwa katika hali ya kutenda. "kila mtu atajua ya kwamba huna hatia"

Genesis 20:17

tasa kabisa

"kutoweza kupata watoto kabisa"

kwa sababu ya Sara, mke wa Abraham

Maana kamili inaweza kuwekwa wazi. "kwa sababu Abimeleki alimchukua mke wa Abrahamu Sara"

Genesis 21

Genesis 21:1

Yahwe akamsikiliza Sara

Hapa msemo "kumsikiliza" una maana ya Yahwe kumsaidia Sara kupata mtoto. "Yahwe alimsaidia Sara"

akamzalia Abrahamu mtoto wa kiume

"akamzaa mtoto wa kiume wa Abrahamu"

katika uzee wake

"Abrahamu alipokuwa mzee sana"

katika muda ule ule ambao Mungu alikuwa amemwambia

"katika muda haswa ambao Mungu alimwambia ingekuja kutokea"

Abrahamu alimuita mwanawe wa kiume, yule ambaye alizaliwa kwake, ambaye Sara alimzaa, Isaka

"Abrahamu alimuita mtoto wake wa kiume, yule ambaye Sara alimzaa, Isaka" au "Abrahamu alimuita mtoto wao wa kiume Isaka"

Abrahamu akamtahiri mwanawe Isaka alipofikisha siku nane

"Mwanae Isaka alipofikisha umri wa siku nane, Abrahamu alimtahiri"

siku nane

"siku 8"

amemwagiza

"alimuamuru Abrahamu kufanya"

Genesis 21:5

mia moja

"100"

Mungu amenifanya nicheke

Sara alikuwa akicheka kwa sababu alishangazwa na alikuwa na furaha. Hii inaweza kuwekwa wazi. "Mungu alinisababisha nicheke kwa furaha"

kila mtu atakaye sikia

Kile ambacho watu wangesikia kinaweza kuwekwa wazi. "kila mtu asikiaye kuhusu kile Mungu amefanya kwangu"

Nani angesema kwa Abraham kwamba Sara atalea mtoto

Hili swali la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Hakuna ambaye angeweza kusema kwa Abrahamu ya kwamba Sara atalea watoto"

atalea mtoto

Hii ni lugha ya upole ikimaanisha kunyonyesha watoto. "mnyonyeshe mtoto maziwa yake mwenyewe"

Genesis 21:8

Mtoto akakua ... Isaka aliachishwa

"aliachishwa" ni lugha ya upole ya kusema mtoto alimaliza kunyonyeshwa. "Isaka akakua, na pale alipokuwa hahitaji tena kunyonya, Abrahamu aliandaa karamu kubwa"

mwana wa Hajiri Mmisri, ambaye alikuwa amezaliwa kwa Abrahamu

Jina la mwana wa Hajiri linaweza kuwekwa wazi. "Ishmaeli, mwana wa Hajiri Mmisri na Abrahamu"

akidhihaki

Inaweza kuwekwa wazi ya kwamba alimzomea au alimcheka Isaka. "alimcheka Isaka"

Genesis 21:10

akamwambia Abrahamu

"Sara akamwambia Abrahamu"

Mfukuze

"mfukuze aende zake" au "mtoweshe"

mwanamke huyu mtumwa pamoja na mtoto wake

Hii ina maana ya Hajiri na Ishmaeli. Sara hakuwatambua kwa majina kwa sababu alikuwa amekasirishwa nao.

pamoja na mwanangu Isaka

"pamoja na mwanangu Isaka"

Jambo hili likamuhuzunisha sana Abrahamu

"Abrahamu alikuwa na huzuni kuhusu kile alichosema Sara"

kwa sababu ya mwanawe

"kwa sababu ilikuwa inahusu mwanawe" Inamaanisha mwanawe, Ishameli"

Genesis 21:12

Usihuzunike kwa sababu ya kijana huyu, na kwa sababu ya mwanamke huyu mtumwa wako

"Usifadhaike kuhusu mvulana na mjakazi wako"

Sikiliza maneno asemayo Sara juu ya jambo hili

Hapa "maneno" yana maana ya kile kinachosemwa. "Fanya kila kitu ambacho Sara anakuambia kuhusu wao"

itakuwa kupitia Isaka kwamba uzao wako utaitwa

Msemo "utaitwa" una maana ya wale watakaozaliwa kupitia Isaka ndio wale Mungu anawatambua kuwa uzao ambao alimuahidi Abrahamu. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Isaka ndiye atakayekuwa baba wa uzao niliokuahidi kwako"

Nitamfanya pia mtoto wa mjakazi kuwa taifa

Neno "taifa" lina maana ya Mungu atampatia uzao mwingi ili kwamba wawe taifa kubwa la watu. "Nitamfanya mwana wa mwanamke mjakazi pia awe baba wa taifa kubwa"

Genesis 21:14

akachukua mkate

Maana zaweza kuwa 1) hii inaweza kumaanisha chakula kwa ujumla au 2) hii ina maana ya mkate mahususi.

kiriba cha maji

"mfuko wa maji". Chombo cha maji kilitengenezwa kwa ngozi ya mnyama.

Maji yalipokwisha kwenye kiriba

"Mfuko wa maji ulipokuwa tupu" au "Walipokunywa maji yote"

umbali kama wa kutupa mshale

Hii ina maana ya umbali ambao mtu anaweza kutupa mshale kwa upinde. Hiini kama mita 100.

nisitazame kifo cha mtoto

Kitenzi hiki cha kujitegemea "kifo" kinaweza kuwekwa kama "kufa". "Sitaki kutazama mwanangu akifa"

akapaza sauti yake akalia

Hapa "sauti" ina maana ya sauti ya kilio chake. "kupaza sauti yake" ina maana ya kulia kwa sauti kubwa. "alipaza kwa sauti kubwa na kulia" au "alilia kwa sauti"

Genesis 21:17

kilio cha kijana

"kilio cha kijana". Hapa "kilio" ina maana ya sauti ambayo kijana alilia au alizungumza. "sauti ya Ishmaeli"

malaika wa Mungu

"mjumbe kutoka kwa Mungu" au "Mjumbe wa Mungu"

kutoka mbinguni

Hapa "mbinguni" ina maana ya sehemu ambapo Mungu huishi.

Nini kinakusumbua

"Tatizo ni nini" au "kwa nini unalia"

kilio cha kijana mahali alipo

Hapa "kilio" ina maana ya sauti ambayo kijana alilia au alizungumza. "sauti ya kijana alipokuwa amelala pale chini"

msimamishe mtoto

"msaidie kijana asimame"

nitamfanya kuwa taifa kubwa

Kumfanya Ishamaeli kuwa taifa kubwa ina maana Mungu atampa uzao mwingi ambao utakua taifa kubwa. "Nitafanya uzao wake kuwa taifa kubwa" au "Nitamfanya awe baba wa taifa kubwa"

Genesis 21:19

Mungu akayafunua macho ya Hajiri

Mungu kumfanya Hajiri aweze kuona kisima inazungumzwa kana kwamba alimfungua macho kihalisia. "Mungu alisababisha Hajiri kuona" au "Mungu alimuonyesha Hajiri"

kiriba

"chombo kilichoundwa na ngozi" au "mfuko"

kijana

"mvulana" au "Ishameli"

Mungu akawa pamoja na kijana

Hapa msemo wa "akawa pamoja" ni lahaja ambayo ina maana ya Mungu alimsaidia au alimbariki mvulana. "Mungu alimuongoza mvulana" au "Mungu alimbariki mvulana"

akawa mwindaji

"akawa na uwezo sana wa kutumia upinde na mishale"

akampatia mke

"akapata mke"

Genesis 21:22

Ikawa kwamba katika wakati ule

Msemo huu unaweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

Fikoli

Hili ni jina la mwanamume.

kamanda wa jeshi lake

"kamanda wa jeshi lake"

jeshi lake

neno "lake" lina maana ya Abimeleki.

Mungu yuko pamoja na wewe katika yote uyatendayo

Hapa msemo "yuko pamoja nawe" ni lahaja yenye maana ya Mungu husaidia au humbariki Abrahamu. "Mungu hubariki kila kitu ufanyacho"

Sasa basi

Neno "Sasa" halimaanishi "katika muda huu", lakini linatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata. "Sasa basi"

niapie hapa kwa Mungu

Hii ni lahaja yenye maana ya kutoa kiapo cha dhati kinachoshuhudiwa na mamlaka ya juu, kwa hali hii ni Mungu. "niahidi mimi na Mungu kama shahidi"

kwamba hutanifanyia baya

"ya kwamba hutanidanganya"

kwamba hutanifanyia baya ... pamoja na uzao wangu

Hii inaweza kuelezwa kwa njia ya chanya. "utanifanyia haki mimi na uzao wangu"

Onesha kwangu ... gano lile lile la uaminifu ambalo nimekuonesha wewe

Wanamume wawili walifanya agano kati yao. Kitenzi kinachojitegemea "umaninifu" kinaweza kuelezwa kama "mwaminifu" au "mtiifu". "Uwe mwaminifu kwangu na kwa nchi kama nilivyokuwa kwako"

kwa nchi

Hapa "nchi" ina maana ya watu. "kwa watu wa nchi"

nina apa

Hii inaweza kuelezwa kwa taarifa iliyoeleweka. "Ninaapa kuwa mwaminifu kwako na kwa watu wako kama ulivyokuwa kwangu"

Genesis 21:25

Abraham pia akamlalamikia Abimeleki

Maana zaweza kuwa 1) Abrahamu alikuwa akilalamika kuhusu kile kilichotokea au 2) "Abrahamu pia alimkaripia Abimeleki"

kuhusu kisima cha maji ambacho watumishi wa Abimeleki wamekinyang'anya

"kwa sababu watumishi wa Abimeleki walichukua kisima kimoja cha visima vya Abrahamu"

wamekinyang'anya kwake

"kuchukua kutoka kwa Abrahamu" au "wamekitawala"

sijalisikia hadi leo hii

"Hii ni mara ya kwanza nimesikia kuhusu jambo hili"

Abrahamu akachukua kondoo na ng'ombe maksai akampatia Abimeleki

Hii ni ishara ya urafiki na ya kwamba Abrahamu amekubali kuweka agano na Abimeleki.

Genesis 21:28

Abraham akatenga wanakondoo wa kike saba peke yao

"Abrahamu aligawanya kondoo saba wa kike kutoka kundini"

saba

"7"

Nini maana ya hawa wanakondoo wa kike saba ambao umewatenga peke yao?

"Kwa nini umegawanya hawa kondoo saba kutoka kundini?"

utawapokea

"utachukua"

kutoka mkononi mwangu

Hapa "mkononi" una maana ya Abrahamu. "kutoka kwangu"

iwe ushahidi

Neno "iwe" ina maana ya zawadi ya kondoo saba.

ili kwamba iwe ushahidi kwangu

Kitenzi kinachojitegemea "shahidi" kinaweza kuelezwa kama "kuthibitisha". "Kuthibitisha kwa kila mtu"

Genesis 21:31

akaita mahali pale

"Abrahamu akapaita mahali pale"

Beerisheba

"Beerisheba inaweza kuwa na maana ya "kisima cha kiapo" au "kisima cha saba".

wote

"Abrahamu na Abimeleki"

Fikoli

Hili ni jina la mwanamume.

wakarudi katika nchi ya Wafilisti

"wakarudi katika nchi ya Wafilisti"

Genesis 21:33

mti wa mkwaju

Huu ni mti wa kijani ambao unaota jangwani. Inaweza kusemwa kwa ujumla zaidi. "mti"

Mungu wa milele

"Mungu aishiye milele"

siku nyingi

Hii ina maana ya muda mrefu zaidi

Genesis 22

Genesis 22:1

Ikawa kwamba

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

baada ya mambo hayo

Msemo huu una maana ya matukio katika sura ya 21.

Mungu akampima Abrahamu

Inasemekana Mungu alimpima Abrahamu kujifunza kama Abrahamu atakuwa mwaminifu kwake. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. Mungu alipima uaminifu wa Abrahamu.

Mimi hapa

"Ndio, nasikiliza" au "Ndio, kuna nini?"

mwanao wa pekee

Inasemekana ya kwamba Mungu anajua ya kuwa Abrahamu ana mtoto mwingine, Ishmaeli. Hii inasisitiza ya kwamba Isaka ni mwana ambaye Mungu alimuahidi kumpa Abrahamu. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "mwana wako wa pekee ambaye nilikuahidi"

umpendaye

Hii inasisitiza upendo wa Abrahamu kwa mwanawe, Isaka.

nchi ya Moria

"nchi inayoitwa Moria"

akatandika punda wake

"akambebesha punda wake" au "akaweka juu ya punda kile kilichohitajika kwa ajili ya safari"

vijana wake

"watumishi"

kisha akapanga safari

"alianza safari yake" au "alianza kusafiri"

Genesis 22:4

Katika siku ya tatu

Neno "tatu" ni nambari ya mpango kwa ajili ya tatu. "Baada ya kusafiri kwa siku tatu"

akaona mahali pakiwa mbali

"akaona kwa mbali sehemu ambayo Mungu alizungumzia"

vijana wake

"watumishi"

Tutaabudu

Neno "tutaabudu" ina maana ya Abrahamu pekee na Isaka.

tutarudi hapa penu

"nitarudi kwako"

akaziweka juu ya Isaka mwanawe

"akamfanya Isaka, mwanawe, kuibeba"

Mkononi mwake

Hapa "mkononi mwake mwenyewe" inasisitiza ya kwamba Abrahamu mwenyewe alibeba vitu hivi. "Abrahamu mwenyewe alibeba"

moto

Hapa "moto" ina maana ya sufuria yenye mkaa unaowaka au tochi au taa. "kitu cha kuanzishia moto"

wote wawili wakaondoka pamoja

"waliondoka pamoja" au "wote wawili waliondoka pamoja"

Genesis 22:7

Baba yangu

Hii ni njia ya upendo ya mwana kuongea kwa baba yake.

Nipo hapa

"Ndio, nasikiliza" au "Ndio, kuna nini?"

Mwanangu

Hii ni njia ya upendo ya baba kuongea kwa mwanawe.

moto

Hapa "moto" ina maana ya sufuria yenye mkaa unaowaka au tochi au taa. "kitu cha kuanzishia moto"

mwanakondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa

"mwanakondoo ambaye utamtoa kama sadaka wa kuteketezwa"

Mungu mwenyewe

Hapa "mwenyewe" inasisitiza ya kwamba Mungu atatoa mwanakondoo.

atatupatia

"atatupatia sisi"

Genesis 22:9

Walipofika mahali

"Abrahamu na Isaka walipofika katika sehemu ile"

akamfunga

"akamfunga kamba"

juu ya madhabahu, juu ya zile kuni

"juu ya kuni zilizokuwa juu ya madhabahu"

akanyoosha mkono wake akachukua kisu

"akaokota kile kisu"

Genesis 22:11

malaika wa Yahwe

Maana zinaweza kuwa 1) Yahwe alijifanya kuonekana kama malaika au 2) huyu alikuwa mmoja wa malaika wa Yahwe au 3) huyu alikuwa mjumbe maalumu kutoka kwa Mungu (baadhi ya wasomi wanadhani alikuwa Yesu). Kwa sababu msemo hauleweki vizuri, ni bora kutafsiri kama "malaika wa Yahwe" kwa kutumia neno la kawaida linalotumika kwa "malaika".

kutoka mbinguni

Hii ina maana ya sehemu ambapo Yahwe anaishi.

Mimi hapa

"Ndio,ninasikiliza" au "Ndio, kuna nini?"

usinyooshe mkono wako juu ya kijana, wala usifanye jambo lolote kumdhuru

Msemo "usinyooshe mkono wako juu ya" ni namna ya kusema "usimdhuru". Mungu alisema kitu kile kile mara mbili kusisitiza ya kwamba Abrahamu hakupaswa kumdhuru Isaka. "usimdhuru kijana kwa njia yoyote ile"

sasa najua ... kwa ajili yangu

Maneno "najua" na "yangu" yana maana ya Yahwe. Unapotafsiri kilichomo ndani ya nukuu, sema kwa namna ambayo Yahwe alitumia maneno ya "najua" na "yangu" alipomaanisha Yahwe.

unamcha Mungu

Hii ina maana ya kumheshimu Mungu kwa undani na kuonyesha heshima hiyo kwa kumtii yeye.

kuona

"kwa sababu ninaona"

hukumzuilia mwanao ... kwa ajili yangu

"haujamshikilia nyuma mwanao ... kwangu" Hii inaweza kusemwa kwa njia ya chanya. "ulikuwa tayari kumtoa mwanao ... kwangu"

mwanao, mwanao wa pekee

Inasemekana ya kwamba Mungu anajua ya kuwa Abrahamu ana mtoto mwingine, Ishmaeli. Hii inasisitiza ya kwamba Isaka ni mwana ambaye Mungu alimuahidi kumpa Abrahamu. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "mwana wako wa pekee ambaye nilikuahidi"

Genesis 22:13

tazama

Neno "tazama" hapa linatuamsha kuvuta nadhari kwa taarifa ya kushangaza inayofuata.

kulikuwa na kondoo mume amenaswa pembe zake kichakani

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "kulikuwa na kondoo dume aliyekwama pembe zake kichakani" au "kulikuwa na kondoo dume aliyekwama kichakani"

akaenda akamchukua kondoo

"Abrahamu alienda kwa kondoo dume na kumchukua"

atatoa ... itatolewa

"atatupatia sisi"

hata leo

"hata sasa". Hii ina maana ya hata katika kipindi ambacho mwandishi alikuwa akiandika kitabu hiki.

itatolewa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Yeye atatoa"

Genesis 22:15

Malaika wa Yahwe

Maana zinaweza kuwa 1) Yahwe alijifanya kuonekana kama malaika au 2) huyu alikuwa mmoja wa malaika wa Yahwe au 3) huyu alikuwa mjumbe maalumu kutoka kwa Mungu (baadhi ya wasomi wanadhani alikuwa Yesu). Kwa sababu msemo hauleweki vizuri, ni bora kutafsiri kama "malaika wa Yahwe" kwa kutumia neno la kawaida linalotumika kwa "malaika".

mara ya pili

Neno "pili" ni namba ya mpango kwa ajili ya mbili

kutoka mbinguni

Hapa neno "mbinguni" lina maana ya sehemu anapoishi Mungu.

na kusema - Hiki ni kiapo cha Yahwe

"na kuzungumza ujumbe huu kutoka kwa Yahwe" au "na kutamka maneno haya ya Yahwe". Hii ni njia ya fasaha ya kusema ya kwamba maneno yanayofuata yanatoka moja kwa moja kwa Yahwe.

Kwa ajili ya nafsi yangu nimeapa

"Nimeahidi na mimi ni shahidi wangu mwenyewe". Msemo "kuapa kwa" una maana kutumia jina la kitu au mtu kama msingi au nguvu ambayo kiapo kinafanyika. Hakuna kitu chenye nguvu zaidi ya Yahwe kuapa kwa jina lake mwenyewe.

umefanya jambo hili

"umenitii"

hukunizuilia mwanao

"hukumzuia nyuma mtoto wako wa kiume". Hii inaweza kuwekwa katika hali ya chanya. "ulikuwa tayari kumtoa mwanao kwangu"

mwanao, mwanao wa pekee

Inaonyesha ya kwamba Mungu anajua ya kuwa Abrahamu ana mtoto mwingine, Ishmaeli. Hii inasisitiza ya kwamba Isaka ni mwana ambaye Mungu alimuahidi kumpatia Abrahamu.

hakika nitakubariki

"hakika nitabariki"

nitakuzidishia uzao wako

Nitasababisha uzao wako kuongezeka tena na tena" au "Nitasababisha uzao wako kuwa mwingi"

kama nyota za angani, na kama mchanga ulioko kwenye ufukwe wa bahari

Mungu alifananisha uzao wa Abrahamu na nyota na mchanga. Kama vile watu wasivyoweza kuhesabu idadi kubwa ya nyota au chembe za mchanga, kwa hiyo kutakuwa na uzao mwingi wa Abrahamu ambao watu wasingeweza kuwahesabu. "zaidi ya kile uwezavyo kuhesabu"

kama nyota za angani

Hapa neno "mbinguni" ina maana ya kila kitu tunachoona juu ya dunia, kujumlisha jua, mwezi na nyota.

watamiliki lango la adui zao

Hapa "lango" linawakilisha mji wote. "Kumiliki lango la adui zake" ina maana ya kuangamiza adui zake. "atawashinda adui zake kabisa"

Genesis 22:18

Taarifa ya Jumla

Malaika wa Yahwe anaendelea kuzungumza na Abrahamu.

mataifa yote ya dunia watabarikiwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mimi, Bwana, nitabariki watu wote wanaoishi mahali pote"

mataifa ya dunia

Hapa "mataifa" ina maana ya watu wa matiafa.

umetii sauti yangu

Hapa "sauti" ina maana ya kile ambacho Mungu alisema. "umetii kile nilichosema" au "umenitii"

Abraham akarejea

Ni Abrahamu pekee aliyetajwa kwa sababu alikuwa baba, lakini imeonekana ya kwamba mwanawe alikwenda naye. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "Abrahamu na mwanawe walirejea"

vijana

"watumishi"

wakaondoka

"waliondoka sehemu ile"

akakaa Beerisheba

Ni Abrahamu pekee aliyetajwa kwa sababu alikuwa kongozi wa familia yake na watumishi wake, lakini imeonekana walikuwa pamoja naye. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "Abrahamu na watu wake alikaa Beerisheba"

Genesis 22:20

Ikawa kwamba baada ya mambo haya

"Baada ya matukio haya". Msemo "mambo haya" una maana ya matukio ya Mwanzo 22:1-19

Abraham aliambiwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "mtu alimwambia Abrahamu"

Milka amemzalia pia watoto

"Milka pia alizaa watoto"

Milka

Hili ni jina la mwanamke

walikuwa ni Usi mzaliwa wa kwanza, Busi ndugu yake

"Jina la mwanawe wa kwanza lilikuwa Usi, na majina ya watoto waliosalia walikuwa Busi ndugu yake"

Usi ... Busi ... Kemueli ... Aramu ...Kesedi, Hazo, Pildasi, Yildashi, na bethueli

Haya yote ni majina ya wanamume. Hawa wote kasoro Aramu walikuwa watoto watoto wa nahori na Milka.

Genesis 22:23

Bethueli akawa baba wa Rebeka

"Baadae Bethueli akawa baba wa Rebeka"

Hawa walikuwa ni wale watoto wanane ambao Milka alizaa kwa Nahori, ndugu yake na Abraham

"hawa walikuwa watoto wanane wa Milka na Nahori, ndugu yake Abrahamu" Hii ina maana ya watoto waliorodheshwa katika 22:20.

nane

"8"

Suria wake

"Suria wa Nahori"

Reuma

Hili ni jina la mwanamke.

pia akamzaa

"pia akajifungua"

eba, Gahamu, Tahashi, na Maaka

Haya yote ni majina ya wanamume

Genesis 23

Genesis 23:1

Sara akaishi mika mia moja na ishirini na saba

miaka saba - 'Sara aliishi miaka 127"

Hii ndiyo ilikuwa ni miaka ya maisha ya Sara

Baadhi ya watafsiri hawajumlishi sentensi hii.

Kiriathi Arba

Hili ni jina la mji.

Abraham akaomboleza na kumlilia Sara

"Abrahamu alikuwa na huzuni sana na akalia kwa sababu Sara alikufa"

Genesis 23:3

akainuka na kutoka kwa mkewe aliye kufa

"akasimama na kuacha mwili wa mke wake"

watoto wa kiume wa Hethi

Hapa "watoto" ina maana ya wale waliotokana na Hethi. "uzao wa Hethi" au "Wahiti"

miongoni mwenu

Wazo hili linaweza kuelezwa kwa lugha ya eneo. "katika nchi yako" au "hapa"

Tafadhari nipatieni mahali

"Niuzie sehemu ya nchi" au "Niruhusu kununua kipande cha nchi"

wafu wangu

Kivumishi kidogo "wafu" kinaweza kuelezwa kama kivumishi au kitenzi. "mke wangu aliyekufa" au "mke wangu ambaye amekufa"

Genesis 23:5

Wana wa Hethi

Hapa "wana" ina maana ya wale waliotokana na Hethi. "uzao wa Hethi"

bwana wangu

Msemo huu unatumika kuonyesha heshima kwa Abrahamu.

mwana wa Mungu

Hii ni lahaja. Hii yaweza kuwa na maana ya "mwanamume mwenye mamlaka" au "kiongozi mwenye nguvu"

wafu wako

Kivumishi kidogo cha "wafu" kinaweza kusemwa kama kitenzi au kwa njia ya urahisi kama "mke". "mke wako ambaye amekufa" au "mke wako"

katika makaburi yetu utakayochagua

"sehemu bora kabisa ya makaburi yetu"

atakaye kuzuilia kaburi lake

"kuzuia sehemu ya makaburi kwako" au " kukataa kukupatia makaburi"

Genesis 23:7

kusujudu

Hii ina maana ya kuinama au kupiga goti chini kabisa kwa kuonyesha unyenyekevu wa heshima na taadhima kwa mtu.

kwa watu wa nchi ile, kwa wana wa Hethi

"kwa wana wa Hethi waliokuwa wakiishi katika eneo lile"

wana wa Hethi

Hapa "wana" ina maana ya wale amabo wametoka kwa Hethi. "uzao wa Hethi"

wafu wangu

Kivumishi kidogo "wafu" kinaweza kuelezwa kama kivumishi au kitenzi. "mke wangu aliyekufa" au "mke wangu ambaye amekufa"

Efroni .... Sohari

Haya ni majina ya wanamume.

pango la Makpela, ambalo analimiliki, ambalo liko mwishoni mwa shamba lake

"pango lake ambalo lipo mwishoni mwa shamba lililoko Makpela"

pango la Makpela

"pango lililoko Makpela". Makpela ilikuwa jina ya eneo au sehemu. Efroni alimiliki shamba katika Makpela na pango ambalo lilikuwa katika shamba.

ambalo analimiliki

Hii inatueleza jambo kuhusu pango lile. Efroni alimiliki pango lile.

ambalo liko mwishoni mwa shamba lake

Hii pia inatumabia jambo kuhusu pango lile. Pango lilikuwa mwishoni mwa shamba la Efroni.

aniuzie waziwazi

"niuzie mbele yenu wote" au "niuzie mbele ya uwepo wenu"

kama miliki

"kama kipande cha nchi ambacho nitamiliki na kutumia"

Genesis 23:10

Sasa Efroni alikuwa ameketi miongoni mwa wana wa Hethi

Hapa "Sasa" inatumika kuweka alama ya badiliko ya habari kwenda kwa taarifa ya nyuma kuhusu Efroni.

Efroni

Hili ni jina la mwanamume.

wana wa Hethi

Hapa "wana" ina maana ya wale ambao wametoka kwa Hethi. "uzao wa Hethi"

alipowasikia wana wa Hethi

Nomino inayojitegemea "alipowasikia" inaweza kuwekwa kama "kusikia" au "kusikiliza". "ili kwamba wana wote wa Hethi waweze kumsikia" au "wakati wana wote wa Hethi walipokuwa wakimsikiliza"

wote ambao walikuwa wamekuja langoni mwa mji wake

Hii inaelezea ni wana wapi wa Hethi walikuwa wakisikiliza. "wale wote waliokusanyika langoni mwa mji"

langoni mwa mji wake

Lango la mji ilikuwa mahali ambapo viongozi wa mji walikutana kufanya maamuzi muhimu.

mji wake

"mji ambao aliishi". Msemo huu unaonyesha ya kwamba Efroni alikuwa wa mji ule. Haimaanishi ya kwamba aliumiliki.

bwana wangu

Huu msemo umetumika kuonyesha heshima kwa Abrahamu.

mbele ya wana wa watu wangu

Hapa "mbele ya" ina maana ya watu waliokuwa kama mashahidi. "pamoja na wananchi kama mashahidi"

wana wa watu wangu

Hii ina maana ya "wananchi wenzangu" au "Wahiti wenzangu"

watu wangu

"watu wangu". Msemo huu unaonyesha ya kwamba efroni alikuwa sehemu ya kundi la watu. Haimaanishi ya kwamba alikuwa kiongozi wao.

Ninakupatia uzike wafu wako

"Ninakupatia. Zika wafu wako"

wafu wako

Kivumishi kidogo "wafu" kinaweza kuelezwa kama kitenzi. "mke wangu aliyekufa" au "mke wangu ambaye amekufa"

Genesis 23:12

akasujudu chini

Hii ina maana ya kuinama au kupiga goti chini kabisa kwa kuonyesha unyenyekevu wa heshima na taadhima kwa mtu.

watu wa nchi

"watu wanaoishi katika eneo lile"

watu wa nchi ile wakisikiliza

Nomino inayojitegemea "wakisikiliza" inaweza kusemwa kama "sikia" au "sikiliza". "ili kwamba watu wanaoishi katika eneo lile waweze kusikia" au "wakati watu waliokuwa wakiishi katika eneo lile wakisikiliza"

ikiwa uko radhi

Neno "lakini" linaonyesha tofauti. Efroni alitaka kutoa shamba kwa Abrahamu; Abrahamu alitaka kulipia. "hapana, lakini kama upo tayari" au "Hapana, lakini kama unakubaliana na hili"

Nitalipia shamba

"Nitakupa fedha kwa ajili ya shamba"

wafu wangu

Kivumishi cha "wafu" kinaweza kuelezwa kama kitenzi au "mke". "Mke wangu aliyekufa" au "mke wangu"

Genesis 23:14

Efroni

Hili ni jina la mwanamume.

Tafadhali bwana wangu, nisikilize

"Nisikie, bwana wangu" au "Nisikilize, bwana mwema"

bwana wangu

Msemo huu unatumika kuonyesha heshima kwa Abrahamu.

Kipande cha ardhi kinathamani ya shekeli mia nne za fedha, na hiyo ni kitu gani kati yangu mimi na wewe?

Efroni alimaanisha ya kwamba kwa kuwa yeye na Abrahamu walikuwa matajiri wote, shekeli 400 za dhahabu zilikuwa kiwango kidogo. Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Kipande cha shamba kina thamani cha shekeli mia nne za fedha tu. Kwako na mimi, hii si kitu"

shekeli mia nne za fedha

Hii ni kama kilogramu 4.5 za fedha

mia nne

"400"

wazike wafu wako

Kivumishi cha "wafu" kinaweza kuelezwa kama kitenzi au "mke". "Nenda kamzike mke wako ambaye amekufa"

Abrahamu akampimia Efroni kiwango cha fedha alizosema

"Abrahamu alipima fedha na kumpatia Efroni kiwango" au "Abrahamu alimhesabia Efroni kiwango cha fedha"

kiwango cha fedha alizosema

"kiwango cha fedha ambacho Efroni alikitaja"

wana wa Helthi wakisikiliza

Nomino inayojitegemea "wakisikiliza" inaweza kusemwa kama "sikia" au "sikiliza". "ili kwamba wana wa Hethi walimsikia" au "wakati wana wa Hethi walikuwa wakisikiliza"

wana wa Helthi

Hapa "watoto" ina maana ya wale waliotokana na Hethi. "uzao wa Hethi"

kwa mujibu wa viwango vya vipimo vya kibiashara

"kwa kutumia viwango vya vipimo vya uzito ambao wafanyabiashara walitumia." Hii inaweza kuelezwa kama sentensi mpya. "Alipima fedha kwa njia ile ile ambayo wafanyabiashara walikuwa wakitumia kupima"

Genesis 23:17

Makpela

Makpela lilikuwa jina la eneo au mahali.

Mamre

Hii ilikuwa jina jingine kwa mji wa Hebroni. Inawezekana iliitwa baada ya Mamre, rafiki yake Abrahamu aliyeishi pale"

shamba pamoja na pango lililokuwamo ndani yake na miti yote

Msemo huu unafafanua kile ambacho mwandishi alimaanisha alipoandika "shamba la Efroni". Halikuwa shamba tu, lakini pia pango na miti katika shamba.

kwa Abraham kwa njia ya manunuzi

"ikawa mali ya Abrahamu alipoinunua" au "ikawa ya Abrahamu baada ya kuinunua"

mbele ya wana wa Hethi

Hapa "mbele ya" ina maana ya watu kutumika kama mashahidi. "pamoja na watu wa Hethi wakitazama kama mashahidi"

wana wa Hethi

Hapa "wana" ina maana ya wale amabo wametoka kwa Hethi. "uzao wa Hethi"

wote waliokuja malangoni pa mji wake

Hii inaeleza ni wana wapi wa Hethi waliomwona Abrahamu akinunua mali ile. "wale wote waliokusanyika langoni mwa mji"

malangoni pa mji wake

Malango ya mji palikuwa pale ambapo viongozi wa mji walikutana kufanya maamuzi muhimu.

mji wake

"mji aliokuwa akiishi". Msemo huu unaonyesha Efroni alikuwa wa mji ule. Haimaanishi ya kwamba aliumiliki.

Genesis 23:19

Baada ya haya

"Alipomaliza kununua shamba lile"

pango la shamba

"pango katika shamba lile"

shamba la Makpela

"shamba katika Makpela"

ambayo ni Hebroni

Maana zaweza kuwa 1) Mamre lilikuwa jina lingine la Hebroni au 2) Hebroni alikuwa akijulikana kama Mamre au 3) Mamre alikuwa karibu sana na mji mkubwa wa Hebroni, kwa hiyo watu waliuita Hebroni mara kwa mara.

kwa Abraham kama milki na eneo la kuzikia

"ikawa mali ya Abrahamu ya makaburi aliponunua kutoka kwa wana wa Hethi"

wana wa Hethi

Hapa "wana" ina maana ya wale amabo wametoka kwa Hethi. "uzao wa Hethi"

Genesis 24

Genesis 24:1

Sasa

Neno hili linatumika hapa kuweka alama ya kuonyesha mapumziko kwa simulizi kuu. Hapa mwandishi anaanza kueleza sehemu mpya ya simulizi.

Weka mkono wako chini ya paja langu

Abrahamu alikuwa akitaka kumuliza mtumishi wake kuapa kufanya jambo. Kuweka mkono chini ya paja la Abrahamu ingeonyesha ya kwamba hakika angefanya kile alichotaka kuapa kukifanya.

nitakufanya uape

Hii inaweza kuelezwa kama amri. "apa"

uape kwa Yahwe

Msemo "uape kwa" una maana ya kutumia jina la kitu au mtu kama msingi au nguvu ambayo kiapo kinafanywa. "niahidi mimi pamoja na Yahwe kama shahidi wako"

Mungu wa Mbingu na Mungu wa nchi

"Mungu wa mbingu na nchi". Maneno "mbingu" na "nchi" yanatumika pamoja kumaanisha kila kitu ambacho Mungu aliumba. "Mungu wakila kitu mbinguni na nchini"

mbingu

Hii ina maana ya sehemu ambayo Mungu anaishi.

kutoka kwa mabinti wa Wakanaani

"kutoka kwa wanawake wa Kanaani" au "kutoka kwa Wakaanani". Hii ina maana ya wanawake wa Kanaani.

miongoni mwao wale nikaao kati yao

"miongoni mwao wale namoishi" Hapa "nikaapo" ina maana ya Abrahamu na familia yake yote na watumishi. "miongoni mwao tunapoishi"

Lakini utakwenda

Hii inaweza kuelezwa kama amri. "Apa ya kwamba utakwenda" au "Lakini ondoka"

ndugu zangu

"familia yangu"

Genesis 24:5

Itakuwaje

"nitafanyaje iwapo"

hatakuwa tayari kufuatana nami

"hatanifuata" au "akikataa kurudi pamoja nami"

Je nitamrudisha mwanao katika nchi ambayo ulitoka

"Je nimchukue mwanao kuishi katika nchi ambayo umetoka"

Hakikisha kwamba hutamrudisha mwanangu kule

Msemo "hakikisha" unasisitiza amri inayofuata. "Kuwa mwangalifu usimpeleke mwanangu kule" au "Hakika hautakiwi kumpeleka mwanangu kule"

ambaye alinitoa mimi kutoka katika nyumba ya baba yangu

Hapa "nyumba" ina maana ya watu katika familia. "aliyenichukua kutoka kwa baba na familia yangu yote"

aliniahidia kwa kiapo maalumu

"aliapa kiapo kwangu"

akisema, 'Nitawapa uzao wako nchi hii,'

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "akisema kwamba angempataia nchi hii kwa uzao wake"

atatuma malaika wake

Maneno "atatuma" na ":wake" yana maana ya Yahwe.

Genesis 24:8

Taarifa ya Jumla:

Mstari wa 8 ni muendelezo wa maelekezo Abrahamu alimpatia mtumishi wake.

Lakini ikiwa mwanamke hatakuwa tayari kukufuata

"Lakini kama mwanamke anakataa kurudi pamoja nami." Abrahamu alikuwa akijibu swali la mtumishi wake kutoka 24:5.

utakuwa huru katika hiki kiapo changu

"utafunguliwa kutoka kwa kiapo ulichokifanya kwangu". Kutokamilisha kiapo inazungumziwa kana kwamba mtu anakuwa huru kutoka kwa kitu ambacho kimemkamata. "hautapaswa kufanya kile ulichoapa kwangu ambcho ulipaswa kufanya"

akaweka mkono wake jini ya paja la Abrahamu bwana wake

Hii ilikuwa ikionyesha ya kwamba hakika angefanya kile alichoapa kufanya.

akaapa kwake

"akafanya kiapo kwake"

kuhusiana na jambo hili

"kuhusu ombi la Abrahamu" au "ya kwamba angefanya kile alichoambiwa na Abrahamu"

Genesis 24:10

na akaondoka. Akachukua pia

Sentensi inayoanza na "Akachukua pia" inatupa taarifa ya nyongeza kuhusu nini mtumishi alichukua katika safari. Alivikusanya kabla ya kuondoka.

Akachukua pia aina zote za zawadi kutoka kwa bwana wake

Hii ina maana alichukua pia vitu vingi ambavyo bwana wake alitaka akawapatie familia ya mwanamke.

Akaondoka na kwenda

"akajiandaa na kuondoka" au "aliondoka na kwenda"

mji wa Nahori

Maana zaweza kuwa 1) "mji ambapo Nahori aliishi" au 2) "mji ulioitwa Nahori".

Akawapigisha magoti ngamia

Ngamia ni wanyama warefu wenye miguu mirefu. Aliwafanya wainamishe miguu yao na kushusha miili yao ardhini. "Aliwafanya ngamia kulala chini"

kisima cha maji

"kisima cha maji" au "kisima"

kuchota maji

"kufuata maji"

Genesis 24:12

Kisha akasema

"Kisha mtumishi akasema"

anijalie kufanikiwa leo na aoneshe agano la uaminifu kwa bwana wangu Abrahamu

Unaweza kuiweka hii kwa neno kiunganishi "kwa". Hii inaonyesha kwa uwazi jinsi mtumishi anataka Mungu amuonyeshe uaminifu wake. "Onyesha agano la uaminifu kwa bwana wangu Abrahamu kwa kunipatia mafanikio leo"

anijalie kufanikiwa

"nipatie mafanikio". Mtumishi alitaka kupata mke mwema kwa mwana wa Abrahamu. Nomino inayojitegemea ya "mafanikio" inaweza kuelezwa kama kitenzi. "nisaidie nifanikiwe" au "nifanye niweze kufanya kile nilichokuja kukifanya"

aoneshe agano la uaminifu kwa bwana wangu Abrahamu

Huu ni uaminifu kwa sababu ya agano ambalo Mungu alifanya na Abrahamu. Nomino inayojitegemea ya "uaminifu" inaweza kuelezwa "uwe mwaminifu". "Uwe mwaminifu kwa bwana wangu Abrahamu kwa sababu ya agano lako"

Tazama

Hapa neno "tazama" linaongeza msisitizo kwa kile kifuatacho.

chemchemi ya maji

"chemichemi" au "kisima"

binti za watu wa mji

"wanawake vijana wa mji ule"

Na itokee kama hivi

"Na itokee kwa namna hii" au "Fanya hii ifanyike"

Nikimwambia msichana, 'tafadhari tua mtungi wako ili niweze kunywa maji,'

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Hii inaweza kuelezwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Ninapomuuliza msichana aniruhusu kunywa maji kutoka kwenye mtungi wake"

tafadhari tua mtungi wako

Wanawake walibeba mitungi juu ya mabega yao. Alitakiwa kushusha na kumpatia mwanamume anywe.

mtungi

chombo cha ukubwa wa kati kilichoundwa na udongo kinachotumika kubeba na kumwaga vimiminikio.

kuwa umeonesha agano la uaminifu kwa bwana wangu

Nomino inayojitegemea "uaminifu" inawezakuelezwa kama "alikuwa mwaminifu". "ya kwamba ulikuwa mwaminifu kwa bwana wangu kwa sababu ya agano lako"

Genesis 24:15

Ikawa kwamba

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama

tazama

Neno "tazama" hapa linatuamsha kusikiliza taarifa ya kushangaza inayofuata.

mtungi

chombo cha ukubwa wa kati kilichoundwa na udongo kinachotumika kubeba na kumwaga vimiminikio.

Rebeka alizaliwa na Bethueli mwana wa Milka, mke wa Nahori, ndugu yake na Abrahamu

"Baba yake Rebeka alikuwa Bethueli. Wazazi wa Bethueli walikuwa Milka na Nahori. Nahori alikuwa kaka yake Abrahamu"

Bethueli

Bethueli alikuwa baba yake Rebeka.

Nahori

Hili ni jina la mwanamume.

Milka

Milka alikuwa mke wa Nahori na mama yake Bethueli.

kashuka kisimani ... na kupanda juu.

Kisima kilikuwa sehemu ya chini katika muinuko wa chini ambapo mtumishi alikuwa amesimama.

Genesis 24:17

kumlaki yule msichana

"kukutana na yule msichana"

maji kidogo

"maji kiasi"

mtungi

chombo cha ukubwa wa kati kilichoundwa na udongo kinachotumika kubeba na kumwaga vimiminikio.

bwana wangu,

"bwana". Hapa mwanamke anatumia msemo huu wa heshima kwa mwanamume, ingawa yeye sio mtumwa wake.

kwa haraka akatua mtungi wake juu ya mkono wake

"alishusha mtungi wake haraka". Alikuwa akibeba mtungi juu ya bega lake. Ilimbidi ahushe ili apate maji kwa ajili ya mtumishi.

Genesis 24:19

Nitachota maji

"Nitafuata maji"

Hivyo akaharakisha akamwaga maji yaliyokuwa mtungini

"Kwa hiyo aliyatoa maji ndani ya mtungi haraka"

chombo cha kunywshea mifugo,

"chombo cha kunywshea wanyama". Chombo cha kunyweshea wanayma ni chombo kilicho wazi kinachoshikilia maji kwa ajili ya wanyama kunywa.

Genesis 24:21

Yule mtu

"Mtumishi"

akamtazama msichana

"akamtazama Rebeka" au "alimtazama yule msichana"

kuona

Kujifunza jambo huwa kunazungumzwa kana kwamba kinaweza kuona. "kujua" au "kukusudia"

amefanikisha njia yake

"Kutimiza lengo la safari yake" au "alifanya safari yake iwe ya mafanikio". Unaweza kuiweka wazi nini mtumishi alijaribu kukusudia. "alimwonyesha mwanamke nani ambaye angekuwa mke wa Isaka"

au la

unaweza kuweka kwa uwazi taarifa inayoeleweka. "au kutofanikiwa katika safari yake"

pete ya pua ya dhahabu yenye uzito wa nusu shekeli

"pete ya pua ya dhahabu ambayo ilikuwa na uzito wa gramu sita". Uzito unaonyesha thamani ya pete hiyo. "pete ya pua ya dhahabu ya gharama"

bangili mbili za dhahabu kwa ajili ya mikono yake zenye uzito wa shekeli kumi

"bangili mbili za dhahabu kwa ajili ya mikono yake zenye uzito wa gramu 110". Uzito unaonyesha ukubwa na thamani yao. "bangili mbili za dhahabu kwa ajili ya mikono yake"

wewe ni binti wa nani

"Nani baba yako"

Je kuna nafasi nyumbani mwa baba yako

"Je kuna nafasi katika nyumba ya baba yako"

kwa ajili yetu

Ni wazi ya kwamba wanamume wengine walikuwa katika safari hii na mtumishi wa Abrahamu. Hapa "yetu" ina maana mtumishi na wale aliokuwa amesafiri pamoja naye.

kupumzika usiku

"kukaa usiku huu" au "kukaa usiku wa leo"

Genesis 24:24

Akamwambia

"rebeka alisema" au "msichan yule alisema"

kwake

"kwa mtumishi"

Mimi ni binti wa Bethueli mwana wa Milka, ambaye alimzaa kwa Nahori

"Bethueli ni baba yangu, na wazazi wake ni Milka na Nahori"

Tunayo malisho tele na chakula

Inaeleweka ya kwamba malisho na chakula yalikuwa kwa ajili ya ngamia. "Tuna malisho na chakula cha kutosha kwa ajili ya ngamia"

kwa ajili yako kulala usiku

"kwa ajili yako kulala usiku" au "ambapo utalala kwa usiku huu"

kwa ajili yako

Hapa "yako" ina maana ya mtumishi na wale aliosafiri naye"

Genesis 24:26

yule mtu

"mtumishi"

akainama chini

Hii ni ishara ya unyenyekevu mbele za Mungu.

hakuacha agano lake la uaminifu na kweli yake mbele ya bwana wangu

"hakuacha kuonyesha agano lake la uaminifu na kweli kwa bwana wangu." Nomino zinazojitegemea "uaminifu" na "kweli" zinaweza kuelezwa kama "kuwa mwaniminfu na mkweli". "ameendelea kuwa mwaminifu na mkweli kwa sababu ya agano lake na bwana wangu"

hakuacha

Hii inaweza kuelezwa kwa namna ya chanya. "anaendelea kuonyesha"

ndugu zake

"familia" au "ukoo"

Genesis 24:28

akakimbia na kwenda kuwaeleza watu wa nyumba ya mama yake

Hapa "nyumba" ina maana ya watu waliokuwa wakiishi katika nyumba ya mama yake. "alikimbia katika nyumba na kumwambia mama yake na kila mtu pale"

mambo yote haya

"kila kitu ambacho kilitokea"

sasa

Neno hili linatumika hapa kuweka alama kuweka mapumziko katika simulizi kuu. hapa mwandishi anaelezea taarifa ya nyuma kuhusu Rebeka. Mwandishi anamtambulisha kaka yake, Labani, katika simulizi.

Akisha kuona hereni ya puani ... na kusikia maneno ya Rebeka dada yake

Mambo haya yalitokea kabla hajakimbia nje kwa mwanamume. Hii inatuambia kwa nini Labani alikimbia nje kwa mwanamume yule.

na kusikia maneno ya Rebeka dada yake, "Hivi ndivyo yule mtu alicho niambia,"

Hii inaweza kuelezwa kama nukuu isiyokuwa moja kwa moja. "alipokuwa amesikia ya kuwa dada yake Rebeka amemwambia nini mwanamume amekisema kwake"

tazama

"naam". Neno "tazama" hapa linaongeza msisitizo kwa kile kinachofuata.

Genesis 24:31

Njoo

"Njoo ndani" au "Ingia"

uliye barikiwa na Yahwe

"wewe ambaye Yahwe amekubariki"

uliye

Hapa neno la "uliye" lina maana ya mtumishi wa Abrahamu.

Kwa nini umesimama nje?

Labani alitumia swali hili kumkaribisha mtumishi wa Abrahamu katika nyumba yake. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Hauhitaji kubaki nje"

Kwa hiyo yule mtu akaingia ndani ya nyumba

Neno "akaingia" linaweza kutafsiriwa kama "akaenda"

kashusha mizigo kutoka kwa wale ngamia

Haipo wazi nani alifanya kazi hii. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mtumishi wa Labani alishusha mizigo kutoka kwa ngamia" au "ngamia walishushwa mizigo"

Ngamia wakapatiwa malisho na chakula, na maji yakatolewa

Hii haisemi nani alifanya kazi hii. Iwapo utaweka hii katika hali ya kutenda basi sema "watumishi wa Labani" kama jambo. "Watumishi wa Labani waliwapa malisho na chakula ngamia, na wakatoa maji"

kuosha miguu yake ... naye

"kwa watumishi wa Abrahamu na wanamume waliokuwa naye kuosha miguu yao"

Genesis 24:33

Wakaandaa

Hapa neno "wakaandaa" lina maana ya watu wa familia ya Labani au watumishi wa nyumbani.

chakula mbele yake

"kumpatia mtumishi chakula"

niseme kile ninacho paswa kusema

"kuzungumza maneno yangu" au "nimekuambia kwa nini nipo hapa"

amekuwa mtu mkuu

Hapa neno "amekuwa" lina maana ya Abrahamu.

amekuwa mkuu

"amekuwa tajiri sana"

Amempatia

Neno "amempatia" lina maana ya Yahwe.

Genesis 24:36

Taarifa ya Jumla:

Mtumishi wa Abrahamu anaendelea kuzungumza kwa familia ya Rebeka.

alimzalia mwana bwana wangu

"alimzaa mtoto wa kiume"

amempatia ... mwanawe

"bwana wangu amempatia ... kwa mtoto wake wa kiume"

Bwana wangu aliniapisha, akisema

"Bwana wangu amenifanya niape ya kwamba nitafanya kile alichonimabia kufanya. Alisema"

kutoka kwa mabinti wa Wakanaani

Hii ina maana ya wanawake wa Kaanani. "kutoka kwa wanawake wa Kaanani" au "kutoka kwa Wakaanani"

ambao kwao nimefanya makazi

"miongoni mwa wale ninamoishi". Hapa "ninamoishi" ina maana ya Abrahamu na familia yake yotena watumishi wake. "miongoni mwa wale tuishipo"

kwa ndugu zangu

"kwa ukoo wangu"

Genesis 24:39

Taarifa ya Jumla:

Mtumishi wa Abrahamu anaendelea kuzungumza kwa familia ya Rebeka.

pengine mwanamke huyo asikubali kufuatana nami

Hili ni jambo ambalo linaweza kutokea. "Je kama mwanamke hatakuja pamoja nami" au "Nitafanyaje iwapo mwanamke huyu hatakuja pamoja nami?"

mbaye ninakwenda mbele yake

Kumtumikia Yahwe inazungumzwa kana kwamba Abrahamu alikuwa akitembea ndani ya uwepo wa Yahwe. "ambaye namtumikia"

atakufanikisha njia yako

"atafanya safari yako kufanikiwa"

ukoo wa baba yangu

"familia"

Lakini utakuwa huru katika kiapo changu ikiwa utafika kwa ndugu zangu na wasikuruhusu kuja naye. Ndipo utakuwa huru katika kiapo changu

Hii ni nadharia tete ambayo Abrahamu alifikiri isingeweza kutokea. Maana zaweza kuwa 1) "Kuna njia moja tu ya kuwa huru na kiapo changu: iwapo utakuja kwa ndugu zangu na hawatakupatia mwanamke kwako, basi utakuwa huru kutoka kwa kiapo changu" au 2) kujengea mstari wa 40, "iwapo utaenda kwa familia ya baba yangu na kumuuliza msichana, utakuwa umefanya kile nilichokuomba ufanye. Iwapo hawatakupatia msichana kwako, basi utakuwa huru kwa kipao ulichoapa kwangu"

Lakini utakuwa huru katika kiapo changu

"utafunguliwa kutoka kwa kiapo ulichofanya kwangu". Kushindwa kutimiza kiapo inazungumzwa kana kwamba mtu yupo huru na kitu kilichomfunga. "hautapaswa kufanya kile ulichoapa kwangu ambacho ungefanya"

ikiwa utafika kwa ndugu zangu

Lugha zinatumia maneno "njoo" na "kwenda" tofauti. "iwapo utafika kwa nyumba ya ndugu zangu" au "utakapokwenda kwa ndugu zangu"

Genesis 24:42

Taarifa ya Jumla:

Mtumishi wa Abrahamu anaendelea kuzungumza kwa familia ya Rebeka.

kisima

"kisima"

niko hapa nimesimama karibu na kisima cha maji

Mtumishi alikatisha kile alichokuwa akimuuliza Mungu kwa kuvuta nadhari ya Mungu kwa pale alipokuwa amesimama.

na iwe kwamba binti ajaye ... nitakayemwambia ... mwanamke atakayeniambia

Mtumishi alirudia kueleza ombi lake, na alikuwa na mambo matatu kusema juu ya mwanamke ambayo alitumaini yangekuja.

kuchota maji

"kuchukua maji"

mtungi

chombo cha ukubwa wa kati kilichoundwa na udongo kinachotumika kubeba na kumwaga vimiminikio.

awe ndiye mwanamke

Mtumishi alikamilisha ombi lake.

Genesis 24:45

Taarifa ya Jumla

Mtumishi wa Abrahamu anaendelea kuzungumza kwa familia ya Rebeka.

kuzungumza moyoni mwangu

Kuomba kimoyo moyo katika akili ya mtu inazungumzwa kana kwamba alikuwa akizungumza ndani ya moyo wake. Neno "moyo" lina maana ya mawazo yake na fikra zake. "kuomba" au"kuomba kimya kimya"

tazama

"naam" au "ghafla". Neno "tazama" hapa linatuamsha kusikiliza taarifa inayoshangaza inayofuata.

mtungi

chombo cha ukubwa wa kati kilichoundwa na udongo kinachotumika kubeba na kumwaga vimiminikio.

akashuka chini kisimani

Msemo "akashuka chini" unatumika kwa sababu kisima kilikuwa sehemu ya chini zaidi ya mahali watumishi walipokuwa wamesimama.

kisimani

"kisima"

akawanywesha ngamia

"wakawapa ngamia maji"

Genesis 24:47

Taarifa ya Jumla

Mtumishi wa Abrahamu anaendelea kuzungumza kwa familia ya Rebeka.

Binti wa Bethueli, Mwana wa Nahori, ambaye Milka alizaa kwake

"Baba yangu Bethueli. Wazazi wake ni Nahori na Milka"

pete ... bangili

Katika simulizi hii, vitu vyote hivi vilikuwa vya dhahabu.

nikainama

Hii ni ishara ya unyenyekevu mbele za Mungu.

ameniongoza katika njia sahihi

"amenileta hapa"

ambaye ameniongoza

Neno la kiunganishi "kwa sababu" linaweza kutumika kuonyesha hii ni sababu mtumishi alimuabudu Mungu. "kwa sababu Yahwe aliniongoza"

ndugu za bwana wangu

Hii ina maana ya Bethueli, mwana wa Abrahamu kaka yake Nahori.

Genesis 24:49

Taarifa ya Jumla:

Mtumishi wa Abrahamu anaendelea kuzungumza kwa familia ya Rebeka.

Kwa hiyo

"Kwa hiyo". Hapa "kwa hiyo" haimaanishi "katika muda huu", lakini unatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimi linalofuata.

ikiwa mko tayari kumfanyia rehema na kweli, niambieni

Namna gani wangeonyesha uaminifu wao na ukweli inaweza kuelezwa kwa uwazi. "niambie kama utakuwa mwaminifu na mkweli kwa bwana wangu kwa kunipatia Rebeka awe mke wa mwana wake"

mko

Neno "mko" ina maana ya Labani na Bethueli.

uaminifu na kweli

Hizi nomino zinazojitegemea zinaweza kuelezwa kama "umanifu na ukweli"

uaminifu wa familia

Huu ni uaminifu wa watu wa familia

Lakini kama sivyo

Taarifa inayoeleweka inaweza kuelezwa kwa uwazi. "Lakini kama haujajiandaa kumtendea bwana wangu kwa uaminifu na ukweli wa familia"

ili kwamba niweze kwenda upande wa kulia, au kushoto

Maana zaweza kuwa 1) kuamua nini cha kufanya kunazungumzwa kana kwamba mtu atageuka upande mmoja au mwingine. "ili kwamba nijue nini cha kufanya" au 2) mtumishi anataka kujua kama anahitaji kusafiri sehemu nyingine. "ili kwamba niendelee na safari yangu"

Genesis 24:50

Bethueli

Huyu alikuwa baba wa Labani na Rebeka.

Jambo hili limetoka kwa Yahwe

"Yahwe alisababisha haya yote kutokea"

hatuwezi kusema kwako aidha neno baya au zuri

Wanasema hawana mamlaka ya kuamua kwamba aliyofanya Mungu ni mema au mabaya. "hatuthubutu kuhukumu kile ambacho Yahwe anatenda"

Tazama

Neno "tazama" hapa linaongeza msisitizo kwa kile kifuatacho.

Rebeka yu mbele yako

"Huyu hapa Rebeka"

Genesis 24:52

maneno yao

"Maneno ya Labani na Bethueli". Hapa "maneno" ina maana ya kile walichosema. "kile ambacho Labani na Bethueli walisema"

akainama mwenyewe chini

Kuinama chini mbele ya Mungu ni ishara ya kumuabudu yeye.

vipande vya fedha na vipande vya dhahabu

"vipande vya fedha na dhahabu" au "vitu vilivyotengenezwa kwa fedha na dhahabu"

zawadi zenye thamani

"zawadi za gharama" au "zawadi za thamani"

Genesis 24:54

yeye na watu aliokuwa nao

"Watumishi wa Abrahamu na wanamume wake"

wakakaa pale mpaka usiku

"walilala pale usiku ule"

walipoamka asubuhi

"waliamka asubuhi iliyofuata"

Niruhusuni niende

"Niruhusu niondoke na kurudi"

kwa siku chache zingine, angalau siku kumi

"angalau siku kumi zaidi"

kumi

"10"

baada ya hapo

"Kisha"

Genesis 24:56

akasema

"Mtumishi wa Abrahamu akasema"

kwao

"kwa kaka wa Rebeka na mama yake"

msinizuie

"Msinikawize" au "Msinifanye nisubiri"

Yahwe amefanikisha njia yangu

Hapa "njia" ina maana ya safari. "Yahwe amefanya nifanikiwe katika lengo la safari yangu"

Niruhusuni niende

"Niruhusu niondoke"

Genesis 24:59

Kwa hiyo wakampeleka dada yao Rebeka

"Kwa hiyo familia ilimpeleka Rebeka"

dada yao

Rebeka alikuwa dada wa Labani. "ndugu yao" au "dada wa Labani"

mtumishi wake wa kike

Hii ina maana ya mtumishi wa kike ambaye alimlisha Rebeka alipokuwa mtoto mchanga, akamtunza alipokuwa mtoto, na alimtumikia.

Dada yetu

Rebeka hakuwa adad kwa kila mtu katika familia yake. Lakini walimuita kwa jinsi hii kuonyesha walimpenda. "Dada yetu Rebeka"

na uwe mama wa maelfu na wa makumi elfu

Hapa "mama" ina maana ya mama. "na uwe mama wa mamilioni wa watu" au "na uwe na uzao mkubwa"

maelfu na wa makumi elfu

Hii ina maana ya idadi kubwa au idadi isiyohesabika.

uzao wako upate kumiliki lango la wale wanao wachukia

Majeshi huvunja katika malango ya miji ya adui zao na kuwashinda watu. "na uzao wako wawashinde kabisa wale wawachukiao"

Genesis 24:61

Kisha Rebeka akasimama, yeye na watumishi wake wakawapakia ngamia

"Kisha Rebeka akasimama, yeye na watumishi wake wakawapakia ngamia"

Hivyo watumishi wakamchukua Rebeka, na wakaenda zao

"Katika njia hii mtumishi wa Abrahamu alimchukua Rebeka pamoja naye na kurudi naye mahali alipotoka"

Nyakati hizo

Neno hili linaweka alama ya kubadili simulizi. Ilikuwa inaeleza juu ya mtumishi kutafuta mke, na sasa itaanza kueleza kuhusu Isaka.

Beerlahairoi

Hili ni jina la maji ya kisima kule Negebu.

Genesis 24:63

Isaka akaenda kutafakari shambani jioni

"jioni moja Isaka alitoka shambani kufikiri". Hii inaweza kuwa muda mrefu baada ya mtumishi na Rebeka kuondoka nyumbani kwake kwa maana walisafiri umbali mrefu.

Alipotazama akaona, natazama, kulikuwa na ngamia wakija!

Hili neno "tazama" hapa linatumasha kusikiliza kwa taarifa ya kushangaza inayofuata. "Alipotazama juu akashangaa kuona ngamia wakija"

Rebeka akatazama

"Rebeka akatazama juu"

akaruka kutoka kwenye ngamia

"alishuka juu ya ngamia haraka"

akachukua shela yake akajifunika

"Kwa hiyo alijifunika uso na shela yake". Hii ni ishara ya heshima na adabu kwa mwanamume atakayemuoa. Maana kamili inaweza kuelezwa wazi.

shela

Kipande cha kitambaa kilichotumika kufunika kichwa cha mtu, mabega na uso.

Genesis 24:66

akamchukua Rebeka, na akawa mke wake

Misemo hii miwili ina maana ya kwamba Isaka alimuoa Rebeka. "na akamuoa Rebeka" au "na akamchukua kama mke wake"

Kwa hiyo Isaka akafarijika

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Kwa hiyo Rebeka alimfariji Isaka"

Genesis 25

Genesis 25:1

Taarifa ya Jumla:

Taarifa kuhusu Abrahamu.

Hawa wote

Hii ina maana ya watu waliotajwa katika mistari ya 2-4.

Genesis 25:5

Abrahamu akampatia Isaka vitu vyote alivyokuwa navyo

"Isaka alirithi kila kitu alichomiliki Abrahamu". Ilikuwa kawaida kwa baba kugawanya utajiri wake alipokuwa mzee na sio kuacha hivyo kwa wengine kufanya baada ya yeye kufariki.

Genesis 25:7

Hizi ndizo zilikuwa siku za miaka ya uhai wake Abrahamu alizoishi, miaka 175

"Abrahamu aliishi miaka 175"

Abrahamu akapumua pumzi ya mwisho na akafa

"Abrahamu alivuta pumzi yake ya mwisho na akafa". Misemo ya "alivuta pumzi ya mwisho" na "akafa" ina maana ya kitu kimoja. "Abrahamu alikufa"

akapumua pumzi ya mwisho

Hii ni njia ya upole ya kusema mtu alikufa.

katika uzee mwema, mzee aliye shiba siku

Misemo hii miwili ina maana moja na inasisitiza ya kwamba Abrahamu aliishi muda mrefu sana. "alipomaliza kuishi muda mrefu na akawa mzee sana"

mzee aliye shiba siku

Kuishi maisha marefu sana inazungumzwa kana kwamba maisha yalikuwa chombo kinachoweza kujaa.

akakusanywa kwa watu wake

Hii ina maana ya kwamba Abrahamu alikufa, nafsi yake ilikwenda sehemu ile ile ndugu zake waliokufa kabla yake. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "aliwaunga familia yake ambao walikuwa wameshakufa"

Genesis 25:9

pango la Makipela, katika shamba la Efroni

Efroni alimiliki shamba Makpela na pango ambalo lilikuwa ndani ya hilo shamba. Abrahamu alinunua shamba lile kutoka kwa Efroni.

Makpela

Makpela lilikuwa jina la eneo au sehemu.

Efroni ... Soari

Haya ni majina ya wanamume.

lililokuwa karibu na Mamre

Makpela ilikuwa karibu na Mamre.

Mamre

Hii ilikuwa jina jingine kwa mji wa Hebroni. Inawezekana iliitwa baada ya Mamre, rafiki yake Abrahamu aliyeishi pale"

Shamba hili Abrahamu alilinunua

"Abrahamu alinunua shamba hili"

watoto wa Hethi

Hapa "wana" ina maana ya wale amabo wametoka kwa Hethi. "uzao wa Hethi"

Abrahamu akazikwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Walimzika Abrahamu"

mwanae

"Mwana wa Abrahamu"

Beerlalahairoi

Jina hili lina maana ya "kisima cha yule aliye hai anionaye mimi"

Genesis 25:12

Na sasa

Hili neno linatumika kutambulisha sehemu mpya ya simulizi na taarifa kuhusu Ishameli.

Genesis 25:13

Taarifa ya Jumla:

Taarifa ya jumla

Hawa ndio walikuwa wana wa Ishimaeli, na haya ndiyo majina yao, kwa vijiji vyao, na katika vituo vyao; Maseyidi kumi na wawili kufuatana na kabila zao

Hii inaweza kuwekwa kama sentensi mbili. "Haya yalikuwa majina ya wana kumi na wawili wa Ishmaeli. Waliongoza kabila ambazo ziliitwa baada yao, na kila mmoja wao alikuwa na vijiji vyao na kambi zao"

kumi na wawili

"12"

Maseyidi

Hapa neno "maseyidi" ina maana ya wanamume waliokuwa viongozi au watawala wa makabila; haimaanishi ya kwamba walikuwa watoto wa mfalme.

Genesis 25:17

Hii ndiyo ilikuwa miaka ya Ishimaeli, miaka 137

"Ishmaeli aliishi miaka 137"

akapumua pumzi yake ya mwisho na akafa

Msemo "akapumua pumzi yake ya mwisho" na "akafa" zina maana moja. "alikufa"

akakusanywa pamoja na watu wake

Hii ina maana ya kwamba ishmaeli alikufa, nafsi yake ilikwenda sehemu ile ile ndugu zake waliokufa kabla yake. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "alijiunga na familia yake ambao tayari walikuwa wamekufa"

Walioshi

"Uzao wake walikaa"

toka Havila mpaka Shuri

"kati ya Havila na Shuri"

Havila

Havila Ilikuwa mahali katika jangwa la Arabia.

kama yule aelekeaye mbele

"katika upande wa"

Waliishi kwa uadui kati yao

Maana zaweza kuwa 1) "hawakuishi kwa amani pamoja" au 2) "waliishi mbali kutoka kwa ndugu zao wengine"

Genesis 25:19

Haya ndiyo yalikuwa matukio kumuhusu Isaka

Sentensi hii inatambulisha habari ya uzao wa Isaka katika Mwanzo 25:19-35:29. "Hii ni habari ya uzao wa Isaka, mwana wa Abrahamu"

umri wa miaka arobaini

"umri wa miaka 40"

alipomuoa Rebeka kuwa mke wake

"alipomuoa Rebeka"

Bethueli

Bethueli alikuwa baba wa Rebeka.

Padani Aramu

Hili lilikuwa jina lingine la eneo la Mesopotamia, ambalo lipo eneo lile lile na Iraq ya sasa.

Genesis 25:21

alikuwa tasa

"hakuwa na uwezo wa kupata mimba"

Rebeka mkewe akabeba mimba

Inaweza kuwekwa wazi ya kwamba Rebeka alikuwa mimba na watoto wawili katika wakati mmoja. "Rebeka, mke wake, akawa mimba na mapacha"

Watoto hawa walipokuwa tumboni mwake wakasumbuka,

"watoto ndani mwake wakaendelea kugusana baina yao" au "Watoto walisukumana dhidi yao wenyewe ndani mwake"

Watoto ... tumboni mwake

Rebeka alikuwa mimba na mapacha.

Akaenda kumuuliza Yahwe kuhusu jambo hili

"Alienda kumuuliza Yahwe kuhusu suala hili". haipo wazi alienda wapi. Inawezekana alienda sehemu ya siri kuomba, au alienda sehemu kutoa sadaka.

Genesis 25:23

akamwambia

"akamwambia Rebeka"

Mataifa mawili ... atamtumikia mdogo

Hii ni lugha ya kishairi.

Mataifa mawili yako katika tumbo lako

Hapa "mataifa mawili" yana maana ya watoto wawili. Kila mtoto atakuwa baba wa taifa moja. "Mataifa mawili yatakuja pamoja kutoka kwa mapacha ndani yako"

na mataifa haya mawili yatatengana ndani yako

Hapa "mataifa mawili" ina maana ya watoto wawili. Kila mtoto atakuwa baba wa taifa moja. Hii inaweza kutafsiriwa kama kitenzi cha kutenda. "na utakapozaa hawa watoto wawili watakuwa wapinzani"

mkubwa atamtumikia mdogo

Maana zaweza kuwa 1) "mkubwa atamtumika mdogo" au 2) "uzao wa mkubwa utamtumikia uzao wa mdogo"

Genesis 25:24

tazama

Neno la "tazama" hapa linaongeza msisitizo kwa kile kifuatacho. "naam"

mwekundu mwili wote kama vazi la nywele

Maana zaweza kuwa 1) ngozi yake ilikuwa nyekundu na alikuwa na nywele nyingi katika mwili wake au 2) alikuwa na nywele nyingi nyekundu katika mwili wake. "nyekundu na yenye nywele kama nguo iliyotengenezwa na nywele ya mnyama"

Esau

"Jina Esau linafanana na neno "nywele"

umeshika kisigino cha Esau

"kushika sehemu ya nyuma ya mguu wa Esau"

Yakobo

"Jina Yakobo lina maana ya "anashika kisigino"

umri wa miaka sitini

"umri wa miak 60"

Genesis 25:27

akawa mwindaji hodari

"akawa hodari katika uwindaji na kuua wanyama kwa chakula"

mtu mkimya

"mtu wa amani" au"mtu asiyekuwa na mambo mengi"

aliye tumia muda wake akiwa katika mahema

Hii inazungumzia kuhusu muda kana kwamba ilikuwa bidhaa ambayo mtu angetumia. "aliyebaki katika mahema sehemu kubwa ya muda"

Kisha

Neno hili linatumika kuweka alama ya kubadili mwelekeo, kutoka katika simulizi kwenda kwa taarifa ya nyuma kuhusu Isaka na Rebeka.

Isaka akampenda

Hapa neno "akampenda" ina maana "alimpendelea" au "kumpenda zaidi"

kwa sababu alikula wanyama ambao alikuwa anawinda

"kwa sababu alikula wanyama ambao Esau aliwinda" au "kwa sababu alifurahia kula wanyama pori ambao Esau alikamata"

Genesis 25:29

Yakobo akapika

Kwa kuwa huu ni mwanzo wa simulizi kuhusu jambo lilitokea kipindi kimoja, baadhi ya watafsiri wanaweza kuanza na msemo wa "Siku moja, Yakobo alipika".

akapika mchuzi

"alichemsha chakula kiasi" au "alipika mchuzi kiasi". Mchuzi ulipikwa kwa dengu za kuchemsha.

akiwa dhaifu kutokana na njaa

"alikuwa dhaifu kwa sababu alikuwa na njaa sana" au "alikuwa na njaa sana"

nimechoka

"Nimechoka kwa sababu ya njaa" au "Nina njaa sana"

Edomu

Jina Edomu lina maana ya "nyekundu"

Genesis 25:31

haki yako ya mzaliwa wa kwanza

"haki ya mwana wa kwanza kurithi sehemu kubwa ya utajiri wa baba yake"

nakaribia kufa

Esau alitiachumvi kuweka msisitizo jinsi alivyokuwa na njaa. "Nina njaa mno nahisi kama vile ntakufa"

Ni nini kwangu haki ya mzaliwa wa kwanza?

Esau alitumia swali kuweka msisitizo ya kwamba kula ilikuwa muhimu zaidi ya haki ya mzawa wa kwanza. Hii inaweza kutafsiriwa kama kauli. "Urithi wangu haunisaidii iwapo nitakufa kwa njaa!"

Kwanza uape kwangu mimi

Kile ambacho Yakobo alimtaka Esau aape kinaweza kuwekwa wazi. "kwanza apa kwangu ya kwamba utaniuzia haki yako ya mzaliwa wa kwanza"

dengu

Haya ni kama maharage, lakini mbegu zake ni ndogo sana, na kama vile tambarare.

Esau akawa ameidharau haki yake

"Esau alionyesha ya kwamba hakuthamini haki yake ya kuzaliwa"

Genesis 26

Genesis 26:1

Basi

Neno hili linatumika kuweka alama kwa sehemu mpya ya simulizi.

njaa ikatokea

"kukawa na njaa" au "kukawa na njaa nyingine"

katika nchi

Unaweza kusema wazi ya kwamba nchi inayozungumziwa. "katika nchi ambayo Isaka na familia yake waliishi"

iliyotokea siku za Ibrahimu

Msemo "katika siku" ina maana ya wakati ambapo Abrahamu alikuwa hai. "ambayo ilitokea wakati wa uhai wa Abrahamu"

Genesis 26:2

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaanza kuzungumza na Isaka.

akamtokea

"akamtokea Isaka"

Usishuke kwenda Misri

Ilikuwa kawaida kuzungumzia kuondoka nchi ya ahadi kama "kushuka chini" kwenda sehemu nyingine.

kwani kwako wewe na uzao wako, nitawapa nchi hii yote

"kwa maana nitakupa nchi hizi zote kwako na kwa uzao wako"

nitatimiza kiapo nilichomwapia Ibrahimu baba yako

"Nitafanya kile nilichoahidi kwa Abrahamu baba yako kukifanya"

Genesis 26:4

Taarifa ya Jumla:

Yahwe anaendelea kuzungumza na Isaka

Nitauzidisha uzao wako

"Nitasababisha uwe na uzao mwingi"

kama nyota za mbinguni

Hii inazungumzia kuhusu uzao wa Isaka kana kwamba walikuwa sawa na idadi ya nyota.

mbinguni

Hii ina maana ya kila kitu juu ya dunia ikijumlisha jua, mwezi na nyota.

mataifa yote ya dunia yatabarikiwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Nitabariki mataifa yote ya dunia"

Abrahamu aliitii sauti yangu na kutunza maelekezo yangu, amri zangu na sheria zangu

Misemo hii "alitii sauti yangu" na "kutunza maelekezo yangu, amri zangu na sheria zangu" zina maana moja. "Abrahamu alinitii na kufanya kila kitu nilichomuamuru kufanya"

aliitii sauti yangu

Hapa "sauti" ina maana ya Yahwe. "Alinitii"

Genesis 26:6

Hivyo Isaka akakaa Gerari

Isaka pekee ndiye aliyetajwa kwa sababu ni kiongozi wa familia, lakini familia yake yote ilikuwa pamoja naye. "Kwa hiyo Isaka na familia yake walikaa Gerari"

Aliogopa kusema

Hapa "aliogopa" ina maana ya hisia isiyofaa inayompata mtu wakati akipata tishio la kudhuriwa kwake au kwa wengine. "Aliogopa kusema"

wamchukue Rebeka

"ili kwamba wamchukue Rebeka"

Tazama, akamwona Isaka

Neno "tazama" linaonyesha ya kwamba kile alichokiona Abimeleki kilimshangaza. "Na alishangazwa kuona ya kwamba Isaka"

akimpapasa Rebeka

Maana zaweza kuwa 1) alikuwa akimgusa kwa njia ambayo mume humgusa mkewake au 2) alikuwa akicheka na kuzungumza pamoja naye kwa namna ambayo mume huzungumza na mkewe.

Genesis 26:9

Abimeleki akamwita Isaka kwake

Yawezekana Abimeleki alimtuma mtu kumwambia Isaka ya kwamba alihitaji kumuona. "Abimeleki alimtuma mtu kumleta Isaka kwake"

Kwa nini ulisema, 'Yeye ni dada yangu?"

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuelezwa kama nukuu isiyokuwa moja kwa moja. "Kwa nini ulisema ya kwamba ni dada yako?"

amchukue

"ili amchukue"

Ni jambo gani hili ulilotufanyia?

Abimeleki alitumia swali hili kumkaripia Isaka. "Haukupaswa kufanya jambo hili kwetu!"

ungeweza kuleta hatia juu yetu

Hii inazungumzia kuhusu kumsababisha mtu kuwa na hatia kana kwamba "hatia" ilikuwa ni kitu kinachowekwa juu ya mtu. "ungeweza kusababisha tuwe na hatia ya kuchukua mke wa mtu"

juu yetu

Hapa "yetu" ina maana ya Abimeleki na watu wake.

Mtu yeyote atakayemgusa mtu huyu

Hapa "atakayemgusa" ina maana ya kumgusa kwa namna ya kumdhuru. "Yeyote atakayemdhuru mwanamume huyu"

hakika atauwawa

Inawezekana Abimeleki alikusudia kumwambia mtu kumuua yeyote ambaye angemdhuru Isaka au Rebeka. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Nitamuua" au "Nitawaamuru wanamume wangu kumuua"

Genesis 26:12

Taarifa ya Jumla

Hii inaanza sehemu mpya ya simulizi. Inabadilisha kutoka kueleza kuhusu Isaka kumuita Rebeka dada yake, na inaanza kuelezea kuhusu jinsi Isaka alivyokuwa tajiri na Wafilisti wakawa na wivu kwake.

katika nchi hiyo

"Gerari"

vipimo mia

Hii ina maana ya "mara mia zaidi ya alivyopanda"/Inaweza kuelezwa kwa ujumla zaidi kama "zao kubwa sana"

Mtu huyo akawa tajiri

"Isaka akawa tajiri" au "Akawa tajiri"

akaongezeka zaidi hata akawa mkuu sana

"na akapata zaidi na zaidi hadi akawa tajiri sana"

kondoo

Hii inaweza kujumuisha mbuzi pia.

familia kubwa

Hapa "familia" ina maana ya wafanya kazi au watumishi. "watumishi wengi"

Wafilisiti wakamwonea wivu

"Wafilisti walikuwa na wivu kwake"

Genesis 26:15

Basi

Hapa neno hili halimaanishi "katika kipindi hiki". Inaonyesha wapi matukio ya simulizi yanapoanzia. Inaweza kutafsiriwa kwa neno unganishi "Kwa hiyo" kuonyesha ya kwamba hii ni tokeo la kilichotokea katika 26:12.

katika siku za Ibrahimu baba yake

Msemo wa "katika siku za" ina maana ya maisha ya mtu. "wakati Abrahamu, baba yake, alipokuwa akiishi"

Abimeleki akamwambia

Maana zaweza kuwa 1) hili ni tukio lingine kumlazimisha Isaka na watu wake kuondoka. "Kisha Abimeleki akasema" au "Hatimaye Abimeleki akasema" au 2) Abimeleki alifanya uamuzi huu kwa sababu aliona ya kwamba watu wake walikuwa na wivu na walitenda uhasama dhidi ya Isaka. "Basi Abimeleki akasema"

nguvu kuliko sisi

"mwenye nguvu zaidi ya sisi"

Hivyo Isaka akaondoka

Isaka pekee ametajwa kwa sababu yeye ni kiongozi, lakini familia yake na watumishi wake walienda naye. "Kwa hiyo Isaka na nyumba yake waliondoka"

Genesis 26:18

Isaka akachimba

Hapa "Isaka" ina maana ya Isaka na watumishi wake. "Isaka na watumishi wake wakachimba"

vilivyokuwa vimechimbwa

"ambao watumishi wa Abrahamu walichimba"

siku za Abrahimu baba yake

Msemo "katika siku za" ina maana ya maisha yote ya binadamu. "ambapo Abrahamu, baba yake, alipokuwa anaishi"

Wafilisiti walikuwa wamevizuia

Hii ndio ilikuwa sababu ya Isaka kuvichimba. Njia kadhaa za kutafsiri hii ni 1) Kwa kuwa hili lilitokea kwanza, sentensi hii inaweza ikaja kabla ya sentensi juu ya Isaka kuvichimba au 2) Sentensi hii inaweza kuanza na "Isaka alifanya hivi kwa sababu Wafilisti waliwazuia"

wamevizuia

"walizijaza na udongo"

Genesis 26:19

maji yaliyokuwakuwa yakibubujika

Msemo huu una maana ya chemichemi ya maji ya asili waliyofunua walipokuwa wakichimba kisima kipya. Ilitoa maji safi ya muendelezo kwa ajili ya kunywa.

Wachungaji

"wanamume wanaotunza mifugo"

Haya ni maji yetu

Hapa "yetu" ina maana ya wafugaji wa Gerari"

Eseki

Watafsiri wanaweza kuongeza maandishi mafupi yanayosema "Jina la Eseki lina maana ya "malumbano" au "mabishano".

Genesis 26:21

Wakachimba

"Kisha watumishi wa Isaka wakachimba"

wakakigombania

"wafugaji wa Gerari walibishana na wafugaji wa Isaka"

hivyo akakiita

"kwa hiyo Isaka akakiita"

Sitina

Watafsiri wanaweza kuweka maandishi mafupi yanayosema. "Jina la Sitna ina maana ya "kupinga" au "kushtaki"

Rehobothi

Watafsiri wanaweza kuongeza maandishi mafupi yanayosema "Jina la Rehobothi lina maana ya "kuweka nafasi kwa ajili ya" au "nafasi wazi".

ametufanyia ... tutafanikiwa

Isaka alikuwa akijizungumzia mwenyewe na nyumba yake.

Genesis 26:23

Kisha Isaka akaenda Beersheba

Hapa "kwenda juu" inaweza kumaanisha kwenda kaskazini. "Isaka aliondoka pale na kwenda Beersheba"

kuvidisha vizazi vyako

"atasababisha vizazi vyako kuongezeka maradufu" au "atasababisha vizazi vyako kuwa wengi sana"

kwa ajili ya mtumishi wangu Abrahimu

"kwa mtumishi wangu Abrahamu" au unaweza kuweka maana yote wazi zaidi. "kwa sababu nilimuahidi mtumishi wangu Abrahamu kuwa nitafanya hili"

Isaka akajenga madhabahu pale

Unaweza kuweka wazi kwa nini Isaka alijenga dhabahu. "Isaka alijenga dhabahu pale kutoa sadaka kwa Yahwe"

akaliita jina la Yahwe

"Kuita" ina maana ya kuomba au kuabudu. Hapa "jina" lina maana ya Yahwe. "aliomba kwa Yahwe" au "alimuabudu Yahwe"

Genesis 26:26

akamwendea

"akaenda kwa Isaka"

Ahuzathi

Hili ni jina la mwanamume.

rafiki yake

Maana zaweza kuwa 1) "rafiki yake Abimeleki" au 2) "mshauri wa Abimeleki"

Fikoli

Hili ni jina la mwanamume.

Genesis 26:28

Nao wakasema

Hii ina maana ya Abimeleki, Ahuzathi na Fikoli. Mmoja wao aliongea na wengine wawili walikubaliana na kile alichosema. Haikumaanisha waliongea kwa wakati mmoja. "mmoja wao alisema"

Tumeona yakini

"Tunajua" au "Tuna uhakika"

Hivyo na tufanye agano

"Kwa hiyo tunataka kufanya agano"

na kama sisi tulivyokutendea vema wewe

Hii inaweza kutafsiriwa kama mwanzo wa sentensi mpya. "Tumetenda mema tu kwako"

umebarikiwa na Yahwe

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Yahwe amekubariki"

Genesis 26:30

Isaka akawaandalia sherehe, na wakala na kunywa

Kula chakula pamoja ilikuwa sehemu ya kufanya agano na mtu mwingine.

akawaandalia

Hapa "akawaandalia" ina maana ya "Abimeleki, Ahuzathi na Fikoli"

wakala

Hapa "wakala" ina maana ya Isaka, Abimeleki, Ahuzathi, na Fikoli. "walikula wote"

Wakaamuka mapema

"Waliamka mapema"

Genesis 26:32

Akakiita kile kisima Shiba

"Kwa hiyo alikiita kisima Shiba". Watafsiri wanaweza kuongeza maandishi mafupi yanayosema "Jina la Shiba linafanana na neno lenye maana ya "kiapo".

Beersheba

Watafsiri wanaweza kuongeza maandishi mafupi yanayosema "Beersheba inaweza kumaanisha "kisima cha kiapo" au "kisima cha saba"

Genesis 26:34

Taarifa ya Jumla

Sehemu kubwa ya Mwanzo 26 inahusu Isaka. Mistari hii inamhusu mtoto wake mkubwa Esau.

arobaini

"40"

akajitwalia mke

"alioa". Unaweza kusema kwa uwazi ya kwamba alioa wanawake wawili. "alioa wake wawili"

Yudithi ... Basemathi

Haya ni majina ya wake wa Esau.

Beeri ... Eloni

Haya ni majina ya wanamume.

Mhiti

"vizazi vya Hethi" au "mzawa wa Hethi"

Wakamhuzunisha Isaka na Rebeka

Hapa "wakamhuzunisha" ina maana ya Yudithi na Basemathi. Kumhuzunisha au kumsikitisha mtu inazungumziwa kana kwamba "huzuni" ni chombo ambacho mtu anaweza kukileta kwa mtu. "Walimfanya Isaka na Rebeka wawe na huzuni" au "Isaka na Rebeka walimsikitisha kwa sababu yao"

Genesis 27

Genesis 27:1

macho yake kuwa mazito

Hii inazungumzia kuhusu kuwa karibu na kupofuka kana kwamba macho yalikuwa taa na mwanga ulikuwa ukitoweka. "alikaribia kupofuka" au "kidogo apofuke"

akamwambia

"Na Esau akajibu"

Mimi hapa

"Nipo hapa" au "Ninasikiliza'

Akamwambia

"Kisha Isaka akasema"

Tazama hapa

Msemo wa "tazama hapa" unaongeza msisitizo kwa kile kinachofuata. "Sikiliza kwa makini"

Sijui siku ya kufa kwangu

Inasemekana Isaka anajua atakufa hivi karibuni. "Naweza kufa siku yoyote toka sasa"

kufa

Hii ina maana ya kifo cha mwili.

Genesis 27:3

Taarifa ya Jumla

Isaka anaendelea kutoa maelekezo kwa mwanae mkubwa Esau.

silaha zako

"vifaa vyako vya kuwindia"

podo lako

Podo ni kasha la kushikilia mishale. "podo lako la mishale"

ukaniwindie mnyama

"winda mnyama pori kwa ajili yangu"

Uniandalie chakula kitamu, aina ile niipendayo

Neno "kitamu" lina maana ya kitu chenye ladha nzuri sana. "Nipikie nyama tamu ninayoipenda"

kukubariki

Kipindi cha Biblie, baba mara nyingi hutamka baraka juu ya watoto wake.

Genesis 27:5

Basi

Neno "basi" linaonyesha badiliko la msisitizo kwa Rebeka na Yakobo.

Rebeka akasikia Isaka alipoongea na Esau mwanawe

"Rebeka alimsikia Isaka akizungumza na mwanawe Esau"

Esau akaenda ... kuja nayo

Neno "kwa hiyo" inaweza kuongezwa kuonyesha ya kwamba Rebeka anazungumza na Yakobo kwa sababu ya kile alichosikia, na anaongea naye wakati Esau ameondoka. "Kwa hiyo Esau alipokuwa ameondoka ...kuja nayo"

na Esau mwanawe ... na Yakobo mwanawe

Esau na Yakobo walikuwa wote wawili watoto wa Isaka na Rebeka. Wanaitwa "mtoto wake" na "mwanawe" kusisitiza ya kwamba mzazi mmoja alimpendelea mtoto mmoja juu ya mtoto mwingine.

Tazama

Msemo "tazama hapa" unaongeza msisitizo kwa kile kinachofuata. "Sikiliza kwa makini"

Akasema, 'Niletee mnyama na unitengenezee chakula kitamu, ili nikile na kukubariki mbele za Yahwe kabla ya kufa kwangu

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kusemwa katika hali isiyo moja kwa moja. Alimwambia Esau "kuwinda mnyama pori, na kumtengenezea nyama tamu anayoipenda". Kisha kabla hajafa, Isaka atambariki Esau mbele ya Yahwe.

'Niletee mnyama

"Niletee mnyama pori utakayemwinda na kumuua"

unitengenezee chakula kitamu

"nipikie nyama tamu ninayoipenda"

kukubariki mbele za Yahwe

"kukubariki mbele ya Yahwe"

kabla ya kufa kwangu

"kabla sijafa"

Genesis 27:8

Taarifaya Jumla

Rebeka anaendelea kuzungumza kwa mtoto wake mdogo Yakobo.

sasa

Hii haimaanishi "katika kipindi hiki" lakini inatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.

usikilize sauti yangu kama ninavyokuagiza

Rebeka alisema "sauti yangu" kumaanisha kile alichokuwa akisema. "unitii na ufanye kile nachokuambia"

nitaandaa chakula kitamu kutokana nao kwa ajili ya baba yako, kwa namna aipendayo

Neno "kitamu" ina maana ya kitu chenye ladha nzuri sana.

Utakipeleka kwa baba yako

"Kisha peleka kwa baba yako"

ili kwamba akile, na kukubariki

"na atakapokila, atakubariki"

kukubariki

Neno "kubariki" lina maana ya baraka maalumu ambayo baba hutamka kwa watoto wake.

kabla hajafa

"kabla hajafa"

Genesis 27:11

mimi ni mtu lain

"Mimi ni mwanamume mwenye ngozi laini" au "Mimi sina manyoya"

nami nitaonekana kama mdanganyifu kwake

"na atafikiri ya kwamba mimi ni muongo" au "atajua ya kwamba ninamdanganya"

nitajiletea laana badala ya baraka

Kulaaniwa au kubarikiwa inazungumziwa kana kwamba laana na baraka ni vitu vinavyowekwa juu ya mtu. "Kisha kwa sababu ya hili, atanilaani na hatanibariki"

Genesis 27:13

Mwanangu, acha laana yoyote iwe juu yangu

"acha laana yako na iwe juu yangu, mwanangu". Kulaaniwa inazungumziwa kana kwamba laana ni kitu kinachowekwa juu ya mtu. "acha baba yako anilaani badala yako, mwanangu"

sikiliza sauti yangu

Rebeka akasema "sauti yangu" kumaanisha kile alichokuwa akizungumza. "utii kile ninachokuambia" au "unitii"

uniletee

"niletee mwanambuzi mchanga"

akaandaa chakula kitamu, kama alichokipenda baba yake

Neno la "kitamu" lina maana ya kitu chenye ladha nzuri sana.

Genesis 27:15

Akamvalisha ngozi ya mwanambuzi katika mikono yake

Ngozi ya mbuzi ilikuwa bado ina manyoya juu yao.

Akaweka katika mikono ya Yakobo kile chakula kitamu na mkate aliokuwa ameuandaa.

"Alimpatia mtoto wake Yakobo chakula kitamy na mkate aliokuwa ameandaa"

Genesis 27:18

akasema

"Na baba yake akajibu" au "Isaka akajibu"

Mimi hapa

"ndio, nasikiliza" au "Ndio, kuna nini?"

nimefanya kama ulivyoniagiza

"Nimefanya kile ulichonimbia kufanya"

sehemu ya mawindo yangu

Neno "windo" lina maana ya wanyama pori ambayo mtu huwinda na kuua.

Genesis 27:20

akamwambia

"Yakobo alijibu"

ameniletea

Hii ni lahaja yenye maana ya kwamba Mungu alisababisha itokee. "alinisaidia kufanikiwa nilipokuwa nawinda"

kama kweli wewe ni mwanangu Esau au hapana

"kama kweli wewe ni mwanangu Esau"

Genesis 27:22

Yakobo akamkaribia Isaka baba yake

"Yakobo alimkaribia Isaka baba yake"

Sauti ni sauti ya Yakobo

Isaka anafananisha sauti ya Yakobo na Yakobo mwenyewe. "Unasikika kama Yakobo"

lakini mikono ni mkikono ya Esau

Isaka analinganisha mikono ya Esau kwa Esau mwenyewe. "lakini mikono yako inaonekana kama mikono ya Esau"

Genesis 27:24

Akasema

Isaka anauliza swali hili kabla hajambariki mwanawe. "Lakini kwanza Isaka alimuuliza Isaka"

nile mawindo yako

Neno "windo" lina maana ya mnyama pori ambaye watu huwinda na kuua.

akanywa

"na Isaka akainywa"

Genesis 27:26

akanusa harufu ya nguo zake na kumbariki

Inaweza kuwekwa wazi ya kwamba nguo zilinuka kama nguo za Esau. "alinusa nguo zake na zilinuka kama nguo za Esau, kwa hiyo Isaka akambariki"

naye akanusa

"na Isaka akanusa"

harufu

"marashi"

na kumbariki

"na kisha akambariki". Hii ina maana ya baraka maalumu ambayo baba hutamka kwa watoto wake.

Tazama, harufu ya mwanangu

Neno "tazama" linatumika kama msemo wa mkazo kumaanisha "ni kweli". Hakika, harufu ya mwanangu"

alilolibariki Yahwe

Hapa neno "alilolibariki" lina maana ya Yahwe alisababisha mambo mazuri kutokea kwenye shamba na ikawa na matunda. "ambayo Yahwe amesababisha kuzaa sana"

Genesis 27:28

Taarifa ya Jumla

Hii ni baraka ya Isaka. Alifikiri alikuwa akizungumza na Esau, lakini alikuwa akizungumza na Yakobo.

akupe

Hapa "akupe" ni katika hali ya umoja na ina maana ya Yakobo. Lakini baraka ingeweza kuhusika kwa vizazi vya Yakobo.

umande wa mbinguni

"umande" ni matone ya maji yanayounda juu ya mimea wakati wa usiku. Hii inaweza kuwekwa wazi. "umande wa usiku kutoka mbinguni kumwagilia mimea yako"

unono wa nchi

Kuwa na nchi yenye mbolea inazungumziwa kana kwamba nchi ilikuwa nene au tajiri. "udongo mzuri kwa ajili ya kuzaa mimea"

wingi wa nafaka na mvinyo mpya

Kama "nafaka" na "mvinyo" havijulikani, vinaweza kuwekwa kwa ujumla zaidi. "chakula na kinywaji kingi"

Genesis 27:29

wakutumikie ... zako

Hapa hivi viwakilishi vipo katika umoja na vina maana ya Yakobo. Lakini baraka pia inalenga vizazi vya Yakobo.

mataifa yainame

Hapa "mataifa" ina maana ya watu. "watu kutoka mataifa yote yainame"

yainame

Hii ina maana ya kuinama na kutoa heshima na taadhima ya unyenyekevu kwa mtu.

Uwe bwana juu ya ndugu zako

"Kuwa bwana juu ya ndugu zako"

ndugu zako ... wana wa mama yako

Isaka anazungumzia baraka hii moja kwa moja kwa Yakobo. Lakini, inahusika kwa vizazvi vya Yakobo ambao watatawala vizazi vya Esau na vizazi vya ndugu yeyote wa Yakobo ambaye anaweza kuwa naye.

na wana wa mama yako wainame chini yako

"na wana wa mama yako watakusujudu"

Kila anayekulaani na alaaniwe

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Na Mungu alaani kila mtu anayekulaani"

kila anayekubariki abarikiwe

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Na Mungu abariki kila mtu anayekubariki"

Genesis 27:30

ametoka mbele ya Isaka baba yake

"ameondoka tu katika hema la Isaka baba yake"

chakula kitamu

"nyama tamu nayoipenda"

baadhi ya mawindo ya mwanao

Hapa "ya mwanao" ilikuwa njia ya upole ya Esau kumaanisha chakula chake mwenyewe alichokiandaa.

mawindo ya mwanao

Neno "windo" lina maana ya wanyama pori ambao watu huwinda kwa ajili ya kula.

kunibariki

Hii ina maana ya baraka maalumu ambayo baba hutamka kwa watoto wake.

Genesis 27:32

akamwambia

"akamwambia Esau"

Isaka akatetemeka

"Isaka akaanza kutetemeka"

aliyewinda mawindo

Windo ina maana ya mnyama pori ambao watu huwinda na kuua.

Genesis 27:34

akalia kwa kilio kikubwa na cha uchungu sana

Uchungu wa Esau ulikuwa sawa na ladha ya kitu kichungu. "alilia kwa sauti kubwa"

amechukua baraka yako

Huu ni msemo wenye maana ya Yakobo alichukua kilichokuwa cha Esau. "Nimembariki badala yako"

Genesis 27:36

Je hakuitwa Yakobo kwa haki?

Esau anatumia swali kuweka msisitizo juu ya hasira yake kwa Yakobo. "Yakobo ni jina sahihi kwa kaka yangu!"

Yakobo

Watafsiri wanaweza kuongeza maandishi mafupi yanayosema: "Jina la Yakobo lina maana ya "yeye akamataye kisigino". Katika lugha ya asili jina la "Yakobo" linatamkika kama neno la "mdanganyifu"

Alichukua ... baraka

Hii inazungumzia kuhusu haki ya mzaliwa wa kwanza kana kwamba ilikuwa kitu ambacho mtu anaweza kukichukua. "Alinidanganya kumpatia mara mbili ya urithia ambayo ningepaswa kupokea kama mzawa wa kwanza!"

sasa amechukua baraka yangu

Hii inazungumzia juu ya baraka kana kwamba ilikuwa kitu ambacho mtu anaweza kuchua. "na sasa amekudanganya kumbariki yeye badala yake"

Je haukuniachia baraka

Esau anajua ya kwamba baba hawezi kumbariki na vitu vile vile alivyombariki Yakobo. Esau anauliza kama kuna kitu kinachosalia kusemwa kwake ambacho Isaka hakusema alipokuwa akimbariki Yakobo.

Je nikufanyie nini mwanangu?

Isaka anatumia swali kuweka msisitizo ya kwamba hakuna kilichobaki atakachofanya. "Hakuna kitu kingine nachoweza kufanya kwako!"

Genesis 27:38

Je hauna hata baraka moja kwa ajili yangu, babangu

Hii inaweza kuelezwa kwa njia ya chanya. "Baba yangu, je hauna baraka moja zaidi kwa ajili yangu"

Genesis 27:39

kumwambia

"akasema kwa Esau"

Tazama

Hii inaongeza msisitizo kwa kile Isaka anachosema baadae. "Sikiliza" au "Vuta nadhari kwa kile nachokwenda kukuambia"

mbali na utajiri wa nchi

Huu ni msemo unaomaanisha nchi yenye rutuba. "mbali na udongo wenye rutuba"

yako ... nawe

Katika 27:39-40 hivi viwakilishi vipo katika umoja na vina maana ya Esau, lakini kile Isaka anachosema pia kinaashiria kwa vizazi vya Esau.

umande juu angani

"umande" ni matone ya maji yanayounda juu ya mimea wakati wa usiku. Hii inaweza kuwekwa wazi. "umande wa usiku kutoka mbinguni kumwagilia mimea yako"

Kwa upanga wako utaishi

Hapa "upanga" ina maana ya vurugu. "Utaiba na kuua watu ili kupata kile unachohitaji kuishi"

utaiondoa nira yake shingoni mwako

Hii inazungumzia juu ya mtu kuwa na bwana kana kwamba utawala wa bwana juu ya mtu ulikuwa ni nira ambayo mtu anaweza kubeba. "utajifanya huru kutoka kwa utawala wake"

Genesis 27:41

Esau akajisemea moyoni

Hapa "moyoni" ina maana ya Esau mwenyewe. "Esau alijisemea mwenyewe"

Siku za maombolezo kwa ajili ya baba yangu zinakaribia

Hii ina maana ya idadi ya siku mtu huomboleza pale ambapo mmoja wa familia anapokufa.

Rebeka akaambiwa maneno ya Esau mwanawe mkubwa

Hapa "maneno" yana maana ya kile Esau alichosema. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mtu alimwambia Rebeka kuhusu mpango wa Esau"

Tazama

"Sikiliza" au "Vuta nadhari"

anajifariji

"anajifanya ajisikie vizuri"

Genesis 27:43

sasa

Hii haimaanishi "katika muda huu", lakini inatumika kuvuta nadhari kwa jambo muhimu linalofuata.

kukimbilia kwa Labani

"ondoka hapa haraka na uende kwa Labani"

kwa muda

"kwa kipindi cha muda"

mpaka hasira ya ndugu yako itakapopungua

"hadi kaka yako atakapopoa"

hata hasira ya ndugu yako itakapokuondokea

Kutokuwa na hasira inazungumziwa kana kwamba hasira hugeukia upande tofauti kutoka kwa mtu. "hadi pale atakapokuwa hana hasira na wewe"

Kwa nini niwapoteze ninyi nyote katika siku moja?

Rebeka anatumia swali kuweka msisitizo juu ya mawazo yake kwa suala hili. "Sitaki kuwapoteza wote wawili katika siku moja!"

niwapoteze ninyi nyote katika siku moja

Inasemekana ya kwamba iwapo Esau atamuua Yakobo, basi watamuua Esau kama muuaji.

niwapoteze

Hii ni njia ya upole inayomaanisha wanawe kufa.

Genesis 27:46

Nimechoka na maisha

Rebeka anatia chumvi kuweka msisitizo jinsi alivyofadhaishwa kuhusu mwanamke Mhiti ambaye Esau alimuoa. "Nimefadhaishwa sana"

binti za Hethi

"hawa wanawake wahiti" au "vizazi vya Wahiti"

kama wanawake hawa, baadhi ya binti za nchi

Msemo "binti wa nchi" ina maana ya wanawake wenyeji. "kama wanawake hawa wanaoishi katika nchi hii"

maisha yatakuwa na maana gani kwangu?

Rebeka anatumia swali kuweka msisitizo jinsi atakavyofadhaishwa iwapo Yakobo atamuoa mwanamke Mhiti". "Maisha yangu yatakuwa mabaya!"

Genesis 28

Genesis 28:1

Usichukuwe

"Usichukue"

Inuka, nenda

"Nenda mara moja"

Padani Aramu

Hili lilikuwa jina lingine kwa ajili ya eneo la Mesopotamia, ambalo lipo eneo sawa na Iraq ya sasa.

nyumba ya

Hii ina maana ya vizazi vya mtu au ndugu wengine. "familia"

Bethueli

Bethueli alikwa baba wa Rebeka.

baba wa mama yako

"babu yako"

mmojawapo wa binti

"kutoka kwa mabinti"

kaka wa mama yako

"mjomba wako"

Genesis 28:3

Taarifa ya Jumla:

Isaka anaendelea kuzungumza na Yakobo

akupe uzao na akuzidishe

Neno "kuongeza" unaelezea jinsi Mungu angemfanya Yakobo "azidishiwe". "akupe uzao na watoto wengi"

Na akupe baraka ya Ibrahimu, wewe, na uzao wako baada yako

Hii inazungumzia kuhusu kubariki mtu kana kwamba baraka ni kitu ambacho mtu anaweza kutoa. Nomino inayojitegemea "baraka" inaweza lusemwa kama "bariki". "Na Mungu akubariki wewe na uzao vyako kama alivyombariki Abrahamu" au "Na Mungu akupatie wewe na uzao wako kile alichoahidi kwa Abrahamu"

kwamba uweze kumilki nchi

Mungu kutoa nchi ya Kaanani kwa Yakobo na uzao wake inazungumziwa kana kwamba mtoto alikuwa akirithi fedha au mali kutoka kwa baba yake.

nchi ambapo umekuwa ukiishi

"nchi ambayo ulikuwa ukiishi"

ambayo Mungu alimpa Abrahamu

"ambayo Mungu aliahidi kwa Abrahamu"

Genesis 28:5

Padani Aramu

Hili lilikuwa jina lingine kwa ajili ya eneo la Mesopotamia, ambalo lipo eneo sawa na Iraq ya sasa.

Bethueli

Bethueli alikwa baba wa Rebeka.

Genesis 28:6

Taarifa ya Jumla:

Simulizi inabadilika kutoka kwa Yakobo kuelekea kwa Esau

Basi

Neno hili linatumiwa hapa kuweka alama ya badiliko kutoka kwa simulizi kwenda kwa taarifa ya nyuma kuhusu Esau.

Padani Aramu

Hili lilikuwa jina lingine kwa ajili ya eneo la Mesopotamia, ambalo lipo eneo sawa na Iraki ya sasa.

kuchukua mke

"kuchukua mke kwa ajili yake"

akaona kwamba Isaka alikuwa amembariki

"Esau aliona pia ya kwamba Isaka alimbariki Yakobo"

Usichukue

"Usichukue"

wanawake wa Kanaani

"binti wa Kaanani" au "wanawake wa Kaanani"

Genesis 28:8

Taarifa ya Jumla:

Hii inaendeleza taarifa ya nyuma kuhusu Esau.

Esau akaona

"Esau akagundua"

wanawake wa Kanaani hawakumpendeza Isaka baba yake

"baba yake Isaka hakuidhinisha wanawake wa Kaanani"

wanawake wa Kanaani

"binti wa Kaanani" au "wanawake wa Kaanani"

Hivyo

"Kwa sababu hiyo"

mbali na wake aliokuwa nao

"kwa kuongeza juu ya wake aliokuwa nao tayari"

Mahalathi

Hili ni jina la mmoja wa binti wa Ishmaeli.

Nebayothi

Hili ni jina la mmoja wa vijana wa Ishmaeli.

Genesis 28:10

Taarifa ya Jumla:

Simulizi inabadilika kurudi kwa Yakobo

Akaja mahali fulani na akakaa pale usiku kucha, kwa kuwa jua lilikuwa limekuchwa

"Akaja katika eneo fulani na kwa sababu jua lilikuwa limezama, aliamua kukaa usiku"

Genesis 28:12

Akaota

"Yakobo alipata ndoto"

imewekwa juu ya nchi

"chini yake ikigusa ardhini"

ilifika hata mbinguni

Hii ina maana ya sehemu ambapo Mungu anaishi.

Tazama

Neno la "tazama" hapa linatuamsha kuvuta nadhari kwa taarifa ya kushtukiza inayofuata.

Yahwe amesimama juu yake

Maana zaweza kuwa 1) "Yahwe alikuwa amesimama juu ya ngazi" au 2) "Yahwe alikuwa amesima kando na Yakobo"

Abrahamu baba yako

Hapa "baba" ina maana ya "babu". "Abrahamu babu yako" au "Abrahamu babu yako"

Genesis 28:14

Taarifa ya Jumla:

Mungu anaendelea kuzungumza na Yakobo ndotoni.

Uzao wako utakuwa kama mavumbi ya ardhi

Mungu analinganisha uzao wa Yakobo na vumbi la ardhi kuweka msisitizo ya idadi kubwa. "Utakuwa na uzao mkubwa zaidi ya utakavyoweza kuhesabu"

na utaenea mbali kuelekea magharibi

Hapa neno "utaenea" lipo katika hali ya upekee lakina lina maana ya uzao wa Yakobo. Inazungumzia kuhusu Yakobo kwa maana yeye ni kiongozi wa familia. "na uzao wako utasambaa hadi magharibi"

na utaenea mbali

Hii ina maana ya watu wataongeza mipaka ya ardhi yao na kukaa

katika maeneo makubwa zaidi.

kuelekea magharibi, mashariki, kaskazini, na kusini Misemo hii inatumika pamoja kumaanisha "pande zote". "katika pande zote"

Kupitia kwako na kupitia uzao wako familia zote za dunia zitabarikiwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Nitabariki familia zote juu ya dunia kupitia kwako na uzao wako"

Tazama

Hii inaongeza msisitizo kwa kile kinachosemwa baadae. "Tazama" au "Sikiliza" au "Vuta nadhari kwa kile nachotaka kukuambia"

kwani sitakuacha. Nitafanya kila

"kwa kuwa sitakuacha mpaka nitende yote"

nitakulinda

"Nitakuweka salama" au "Nitakulinda"

Nitakurudisha katika nchi hii tena

"Nitakuleta katika nchi hii"

Genesis 28:16

akaamka katika usingizi

"aliamka kutoka katika usingizi wake"

nyumba ya Mungu ... lango la mbinguni

Msemo wa "lango la mbinguni" linaelezea ya kwamba sehemu hii ni kiingilio cha "nyumba ya Mungu" na "mlango wa mahali Mungu anapoishi"

Hili ni lango la mbinguni

Hii inazungumzia kuhusu mlango ambapo Mungu anaishi kana kwamba ilikuwa ni ufalme halisi ambao ulikuwa na lango ambalo mtu anatakiwa kufungua kuruhusu watu ndani.

Genesis 28:18

nguzo

Hii ni nguzo ya kumbukumbu, yaani, jiwe kubwa au jabali lililowekwa mwishoni pake.

kumimina mafuta juu yake

Tendo hili linaashiria ya kwamba Yakobo anaweka wakfu nguzo kwa Mungu. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "alimwaga mafuta juu yake ili kuiweka wakfu nguzo kwa Mungu"

Betheli

Watafsiri wanaweza kuongeza maandishi mafupi yanayosema "Jina la Betheli lina maana 'nyumba ya Mungu."

Luzu

Hili ni jina la mji.

Genesis 28:20

akatoa nadhiri

"akafanya kiapo" au "alimuahidi Mungu kwa dhati"

Ikiwa Mungu atakuwa ... ndipo Yahwe atakapokuwa Mungu wangu

Yakobo anazungumza na Mungu katika lugha ya mtu wa utatu. Hii inaweza kusemwa katika lugha ya upili wa mtu. "Iwapo uta ... basi wewe, Yahwe, utakuwa Mungu ambaye nitamuabudu"

katika njia nipitayo

Hii ina maana ya safari ya Yakobo kutafuta mke na kurudi nyumbani. "katika safari hii"

atanipa mkate wa kula

Hapa "mkate" una maana ya chakula kwa ujumla.

katika nyumba ya baba yangu

Hapa "nyumba" ina maana ya familia ya Yakobo. "kwa baba yangu na familia yangu iliyosalia"

jiwe takatifu

Hii ina maana ya kwamba jiwe litaweka alama ya sehemu ambayo Mungu alijitokeza kwake na itakuwa sehemu ambapo watu watamuabudu Mungu. "nyumba ya Mungu" au "sehemu ya Mungu"

Genesis 29

Genesis 29:1

watu wa mashariki

Hii ina maana ya watu wa Paddani Aramu, ambayo ni nchi mashariki mwa nchi ya Kaanani.

na, tazama, makundi matatu ya kondoo yalikuwa yamelala kando yake

Neno "tazama" linaweka alama ya mwanzo wa tukio lingine katika simulizi kubwa.

Kwani kutoka katika hicho kisima

"Kwani kutoka katika kisima hicho". Msemo huu unaweka alama ya badiliko kutoka kwa simulizi kwenda kwa taarifa ya nyuma kuhusu jinsi wafugaji waliwanywesha mifugo"

wangeyanywesha

"wafugaji wangewanywesha" au "wale waliokuwa wakitunza kondoo wangewanywesha"

mdomo wa kisima

Hapa "mdomo" ni njia ya kuelezea uwazi. "uwazi wa kisima"

Genesis 29:4

Yakobo akawambia

"Yakobo aliwaambia wafugaji"

Ndugu zangu

Hii ni njia ya upole ya kumsalimia mgeni.

Labani mwana wa Nahori

Hapa "mwana" ina maana ya uzao wa kiume. Maana nyingine yaweza kuwa "Labani mjukuu wa Nahori".

na, tazama pale, Raheli binti yake anakuja na kondoo

"Tazama sasa! Raheli binti yake anakuja na kondoo"

Genesis 29:7

ni mchana

"jua bado lipo juu angani" au "jua bado linawaka kwa mwanga"

wakati wa kukusanya kondoo pamoja

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "kwako kukusanya mifugo"

kukusanya pamoja

Hii ina maana ya kuwakusanya pamoja ndani ya uzio ili wakae kwa usiku. Maana kamili ya hii inaweza kuwekwa wazi.

kuwaacha wachunge

"waache wale nyasi shambani"

Hatuwezi kuwanywesha

"Inatubidi kusubiri ili kuwanywesha". Hii inahusu suala la muda, na sio ruhusa.

Hatuwezi kuwanywesha mpaka makundi yote yakusanyike pamoja

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "hadi pale wafugaji wengine watakapokusanya mifugo yao"

kutoka mlangoni mwa kisima

Hapa "mlangoni" ni njia ya kuelezea uwazi. "kutoka kwa kisima" au "kutoka kwa uwazi wa kisima"

na ndipo tutakapowanywesha kondoo

"kisha tutawanywesha kondoo"

Genesis 29:9

kaka wa mama yake

"mjomba wake"

mlangoni mwa kisima

Hapa "mdomo" ni njia ya kuelezea uwazi. "kisima" au "uwazi wa kisima"

Genesis 29:11

Yakobo akambusu Raheli

Nyakati za kale Mashariki ya Karibu, ilikuwa kawaida kumsalimu ndugu na busu. Ingawa, inafanywa baina ya wanamume.

akalia kwa sauti

Yakobo analia kwa sababu amefurahi sana. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi.

ndugu wa baba yake

"ana undugu na baba yake"

Genesis 29:13

mwana wa dada yake

"mpwa wake"

akamkumbatia

"alimkumbatia"

akambusu

Nyakati za kale Mashariki ya Karibu, ilikuwa kawaida kumsalimu ndugu na busu. Ingawa, inafanywa baina ya wanamume.

Yakobo akamwambia Labani mambo haya yote

"kisha Yakobo alimwambia Labani kila kitu alichomuambia Raheli"

mfupa wangu na nyama yangu

msemo huu una maana zinaoana moja kwa moja. "ndugu yangu" au "mmoja wa familia yangu"

Genesis 29:15

Je unitumikie bure ... ndugu yangu?

Labani anatumia swali kusisitiza ya kwamba anatakiwa kumlipa Yakobo kwa kumtumika. Swali linawezakutafsiriwa kama kauli. Pia linaweza kuwekwa katika njia ya chanya. "Hakika ni sahihi ya kwamba nikulipe kwa kunitumikia ingawa wewe ni ndugu yangu."

Basi Labani alikuwa

Neno "basi" linatumika hapa kuweka alama ya badiliko kutoka kwa simulizi kwenda kwa taarifa ya nyuma kuhusu Labani na binti zake"

Macho ya Lea yalikuwa dhaifu

Maana zaweza kuwa 1) "Macho ya Lea yalikuwa mazuri" au 2) "Macho ya Lea yalikuwa ya kawaida"

Yakobo alimpenda Raheli

Hapa neno "alimpenda" lina maana ya mvuto wa kimahaba kati ya mwanamume na mwanamke.

Genesis 29:19

kuliko kumpa mwanamume mwingine

"kuliko kumpa kwa mwanamume mwingine"

nayo ilionekana kwake kama siku chache tu

"lakini muda ulionekana kwake kama siku chache tu"

kwa ajili ya upendo aliokuwa nao kwake

"kwa ajili ya upendo aliokuwa nao kwake" au "kwa sababu ya upendo wake kwake"

Genesis 29:21

Nipe mke wangu, kwani siku zangu zimetimia

Hapa "siku" ina maana ya muda mrefu zaidi. Msemo "zimetimia" unaweza kuwekwa katika hali ya chanya. Kauli hii ina mkazo. Nipatie Raheli ili kwamba niweze kumuoa, kwa maana nimekufanyia kazi miaka saba!"

kuandaa sherehe

"kuandaa sherehe ya harusi". Yawezekana Labani alikuwa na watu walioandaa sherehe hii. "alikuwa na watu waliondaa sherehe ya harusi"

Genesis 29:23

aliyelala naye

Inadokezwa ya kwamba Yakobo hakujua alikuwa na Lea kwa sababu ilikuwa giza na hakuweza kuona. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi.

Labani akampa mtumishi wake wakike Zilpa ... mtumishi wake

Hapa mwandishi anatoa taarifa ya nyuma kuhusu Labani kumpa Zilfa kwa Lea. Inawezekana alimpa Zilfa kwa Lea kabla ya harusi.

Zilpa

Hili ni jina la mtumishi wa Lea.

tazama, kumbe ni Lea

"Yakobo alishangazwa kuona ilikuwa ni Lea kitandani pamoja naye". Neno "tazama" hapa linaonyesha ya kwamba Yakobo alishtushwa na kile alichokiona"

Ni nini hiki ulichonifanyia?

"Yakobo alishangazwa kuona alikuwa Lea kitandani pamoja naye." Neno "tazama" hapa linaonyesha ya kwamba Yakobo alishtushwa na kile alichoona.

Je sikukutumikia kwa ajili ya Raheli?

Yakobo anatumia maswali haya kuonyesha maumivu yake ya kwamba Labani alimdanganya. Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Nimekutumikia kwa miaka saba kumuoa Raheli"

Genesis 29:26

Siyo utamaduni wetu kumtoa

"Huwa hatutoi kwenye familia yetu"

Timiza juma la bibi arusi

"Kumaliza kusherehekea harusi ya Raheli"

na tutakupa yule mwingine pia

Maana kamila inaweza kuwekwa wazi. "na wiki ijayo tutakupatia Raheli pia"

Genesis 29:28

Yakobo akafanya hivyo, na akatimiza juma la Lea

"Na Yakobo akafanya alichosema Labani, na akamaliza kusherehekea wiki ya harusi ya Lea"

Bilha

Hili ni jina la mtumishi wa kike wa Raheli.

Yakobo akalala na Raheli

Hii ni njia ya ustarabu ya kusema kuwa walikutana kimwili. "Yakobo akamuoa Raheli"

akampenda Raheli

Hii inamaanisha upendo wa kimahaba kati ya mwanamme na mwanamke.

Genesis 29:31

Lea hakupendwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Yakobo hakumpenda Lea"

hakupendwa

Hii ni kuza jambo kusisitiza kuwa Yakobo alimpenda Raheli zaidi ya Lea. "alimpenda kwa uhafifu kuliko Raheli"

hivyo akalifungua tumbo lake

Mungu kumsababisha Lea kuwa na uwezo wa kuwa na mimba inazungumziwa kama kwamba Mungu alifungua tumbo lake.

hakuwa na mtoto

"hakuweza kuwa mjamzito"

Lea akashika mimba na kuzaa mwana

"Lea alipata mimba na kumzaa mwana wa kiume"

naye akamwita Rubeni

Jina Rubeni linamaanisha "Tazama, mwana wa kiume."

Yahwe ameliangalia teso langu

Lea alipitia uchungu wa hisia kwa sababu Yakobo alimkataa.. Nomino "teso" inaweza kuwekwa kama kitenzi. "Yahwe aliona kuwa nateseka"

Genesis 29:33

Kisha akashika mimba

"Lea akawa mjamzito"

kuzaa mwana

"akazaa mwana wa kiume"

Yahwe amesikia kwamba sipendwi

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Yahwe amesikia kuwa mme wangu hanipendi"

akamwita Simoni

Jina Simoni linamaanisha "kusikiwa."

mume wangu ataungana nami

"mume wangu atanikumbatia"

nimemzalia wana watatu

"nimezaa wana watatu wa kiume kwa ajili yake"

akaitwa Lawi

Jina Lawi linamaanisha "ambatishwa."

Genesis 29:35

Akashika mimba tena

"Lea akawa na mimba tena"

kuzaa mwana

"Akazaa mwana wa kiume"

akamwita jina lake Yuda

Jina Yuda linamaanisha "sifa."

Genesis 30

Genesis 30:1

Raheli alipoona kwamba hamzalii Yakobo watoto

"Wakati Raheli alipogundua ya kwamba hawezi kupata mimba"

nitakufa

Raheli anatumia ukuzaji kuonyesha jinsi alivyohuzunika ya kuhusu kutopata watoto. "Nitajisikia sina maana yoyote kabisa"

Nipe watoto

"Nisababishie kupata mimba"

Hasira ya Yakobo ikawaka juu ya Raheli

Hasira ya Yakobo inazungumziwa kana kwamba ilikuwa moto. "Yakobo alimkasirikia sana Raheli"

Mimi ni badala ya Mungu, aliyekuzuilia usipate watoto?

Hili ni swali la balagha ambalo Yakobo anatumia kumkaripia Raheli. Inaweza kutafsiriwa kama kauli. "Mimi si Mungu! Mimi siye ninayekuzuia kupata watoto"

Genesis 30:3

Akasema

"Raheli akasema"

Tazama

"Sikiliza" au "Vuta nadhari kwa kile nachotaka kukuambia". Hii inaongeza msisitizo kwa kile Raheli anachosema baadae"

kuna mjakazi wangu Bilha ... nami nitapata watoto kwake

Katika kipindi hicho, njia hii ilikuwa inakubalika kwa mwanamke tasa kupata watoto ambao kisheria wangekuwa wa kwake. Maana kamili inaweza kuwekwa wazi.

Bilha

Hili ni jina la mtumishi wa kike wa Raheli.

magotini pangu

Hii ni namna ya kusema ya kwamba mtoto ambaye Bilha anamzaa atakuwa wa Raheli. "wa kwangu"

nami nitapata watoto kwake

"na kwa njia hii atanifanya niwe na watoto"

Genesis 30:5

Bilha

Hili ni jina la mtumishi wa kike wa Raheli.

kumzalia Yakobo mwana

"akazaa mtoto wa kiume kwa Yakobo"

akamwita jina lake

"Raheli akmpatia jina"

akamwita jina lake Dani

"Jina la Dani lina maana ya "alihukumu".

Genesis 30:7

Bilha ... akashika mimba tena

"Bilha ... akawa mimba tena"

na kumzalia Yakobo mwana wa pili

"na akazaa mtoto wa kiume wa pili kwa Yakobo"

Kwa mashindano yenye nguvu nimeshindana na dada yangu

Msemo huu "mashindano nimeshindana" ni msemo unaotumiwa kwa msisitizo. Pia ni sitiari inayozungumzia jaribio la Raheli kupata mtoto kama dada yake kana kwamba alikuwa akigombana kimwili na Lea. "nimepambana sana kupata watoto kama dada yangu, Lea"

na kushinda

"na nimeshinda" au "nimefaulu"

Akamwita jina lake Naftali

"Jina la Naftali lina maana ya 'mapambano yangu'"

Genesis 30:9

Lea alipoona kwamba

"Lea alipopata ufahamu wa jambo hilo"

akamchukua Zilpa, mjakazi wake, na kumpa Yakobo kama mke wake

"alimpatia Zilpa, mtumishi wake, kwa Yakobo kama mke"

Zilpa

Hili ni jina la mtumishi wa kike wa Lea.

akamzalia Yakobo mwana

"akazaa mtoto wa kiume kwa Yakobo"

Hii ni bahati njema!

"Bahati gani!" au "Bahati gani hii!"

akamwita jina lake Gadi

"Jina la Gadi lina maana ya "mwenye bahati"

Genesis 30:12

Zilpa

Hili ni jina la mtumishi wa kike wa Lea.

akamzalia Yakobo mwana wa pili

"akazaa mtoto wa pili wakiume kwa Yakobo"

Nina furaha!

"Jinsi nilivyobarikiwa!" au "Jinsi nilivyo na furaha!"

mabinti

"wanawake" au "wanawake wadogo"

akamwita jina lake Asheri

"Jina la Asheri lina maana ya "furaha"

Genesis 30:14

Rubeni akaenda

"Rubeni alitoka nje"

Siku za mavuno ya ngano

Hapa msemo "siku za" ni sitiari yenye maana ya majira au kipindi cha mwaka. "katika kipindi cha mwaka cha mavuno ya ngano" au "wakati wa mavuno ya ngano"

tunguja

Hili ni tunda ambalo linasemekana kuongeza uwezo wa kuzaa na kuongeza hamu ya mtu kulala na mpenzi wake. "tunda la upendo"

Je ni jambo dogo kwako ... mme wangu?

"Je haujali ... mume wangu?" Hili ni swali la balagha limetumika kumkaripia Raheli. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli, "ni mbaya sana .. mume wangu"

Je na sasa unataka ... pia?

Hili ni swali la balagha limetumika kumkaripia Raheli. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli, "Na sasa unataka ... pia?"

Basi atalala nawe

"Basi Yakobo atalala" au "Basi nitamruhusu Yakobo alale"

Genesis 30:16

kwa tunguja za mwanangu

"kwa bei ya tunguja za mwanangu"

akashika mimba

"akawa mimba"

na kumzalia Yakobo mwana wa tano

"na akazaa mtoto wa kiume wa tano kwa Yakobo"

Mungu amenipa ujira wangu

Mungu kumzawadia Lea inazungumzwa kana kwamba alikuwa bosi anayelipa mshahara kwa mtu anayefanya kazi kwake. "Mungu amenipa stahiki yangu" au "Mungu amenizawadia"

Akamwita jina lake Isakari

"Jina la Isakari lina maana ya "kuna dhawabu"

Genesis 30:19

Lea akashika mimba tena

"Lea akawa mimba tena"

na kuzaa mwana wa sita kwa Yakobo

"na kuzaa mtoto wa kiume wa sita kwa Yakobo"

Akamwita jina lake Zabuloni

"Jina la Zabuloni lina maana ya "heshima"

na kumwita jina lake Dina

Hili ni jina la binti wa Lea.

Genesis 30:22

Mungu akamkumbuka Raheli na kumsikiliza

Msemo huu "akamkumbuka" una maana kukumbuka. Hii haimaanishi Mungu alimsahau Raheli. Ina maana alimfikiria juu ya ombi lake. "Mungu alimfikiria Raheli na kumpatia kile alichokitaka"

Mungu ameiondoa aibu yangu

Mungu kusababisha Raheli kutosikia aibu tena inazungumziwa kana kwamba "aibu" ni kitu ambacho mtu anaweza kukichukua kutoka kwa mtu mwingine. Nomino inayojitegemea "aibu" inaweza kuwekwa kama "kuona aibu". "Mungu amenisababishia nisione aibu tena"

Akamwita jina lake Yusufu

"Jina la Yusufu maana yake ni "na aongeze"

Yahwe ameniongeza mwana mwingine

watoto wa kwanza wa Raheli walitokana na mtumishi wa kike wa Bilha.

Genesis 30:25

Baada ya Raheli kumzaa Yusufu

"Baada ya Raheli kumzaa Yusufu"

na uniache niondoke

"ili niondoke"

unafahamu nilivyokutumikia

Yakobo anamkumbusha Labani kuhusu mkataba wake (29:26) Nomino inayojitegemea "huduma" inaweza kusemwa kama "kutumika". "unafahamu ya kwamba nimekutumikia muda wa kutosha"

Genesis 30:27

Labani akamwambia

"Labani akamwambia Yakobo"

Ikiwa nimepata kibali machoni pako

Msemo wa "machoni pako" ni lugha inayomaanisha mawazo na maoni ya Yakobo. Iwapo nimepata kibali na wewe" au "Iwapo unapendezwa na mimi"

nimepata kibali

Hii ni lahaja yenye maana ya mtu amekubalika na mtu mwingine.

subiri, kwa sababu

"tafadhali kaa, kwa sababu"

nimejifunza kwa kutumia uaguzi

"Nimegundua kwa desturi yangu ya kiroho na uchawi"

kwa ajili yako

"kwa sababu yako"

Taja ujira wako

Hii inaweza kuwekwa wazi. "Niambie nahitaji kukulipa kiasi gani kukuweka hapa"

Genesis 30:29

Yakobo akamwambia

"Yakobo alimwambia Labani"

jinsi ambavyo mifugo wako wamekuwa nami

"jinsi mifugo wako walivyokuwa vizuri tangu nimeanza kuwatunza"

Kwani walikuwa wachache kabla sijaja

"mifugo wako walikuwa wadogo kabla sijakutumikia"

na wameongezeka kwa wingi

"lakini sasa utajiri wako umeongezeka sana"

Je ni lini mimi nitaandaa kwa ajili ya nyumba yangu pia?

"Basi ni lini nitatunza familia yangu?" Yakobo anatumia swali kuweka msisitizo ya kwamba anataka kujitoa kwa familia yake. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli. "basi ninataka kutunza familia yangu!"

Genesis 30:31

Je nikulipe nini

"Nitakulipa nini" au "Nikupatie nini". Hii inaweza kuwekwa wazi zaidi. "Nitakulipa nini ili kwamba ubaki na kunitumikia"

Ikiwa utafanya jambo hili kwa ajili yangu

Neno la kiunganishi "ikiwa" inaweza kuongezwa kuonyesha ya kwamba hili ni jambo moja ambalo Yakobo anataka. "Ikiwa utafanya jambo hili kwa ajili yangu"

nitawalisha tena kondoo wako na kuwatunza

"nitalisha na kuwatunza mifugo wako"

kuondoa kila kondoo mwenye milia na mabaka, na kila kondoo mweusi kati yao, na kati ya wenye mabaka na milia katika mbuzi

"na kutoa kila kondoo wa madoia, kila kondoo mweusi, na kila mbuzi mwenye madoa"

Hawa watakuwa ujira wangu.

"Hii itakuwa gharama ya kuniweka hapa"

Genesis 30:33

Uadilifu wangu utashuhudia kwa ajili yangu hapo baadaye

Neno "uadilifu" lina maana ya "uaminifu". Hii inazungumzia kuhusu uadilifu kana kwamba ni mtu ambaye anaweza kushuhudia kwa ajili au dhidi ya mtu mwingine. "Na baadae utajua kama nimekuwa mwaminifu na wewe au la"

Kila ambaye hana milia na hana madoa miongoni mwa mbuzi, na mweusi kati ya kondoo, ikiwa wataonekana kwangu, watahesabiwa kuwa wameibwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Iwapo utakuta mbuzi yeyote asiyena madoa au kondoo yeyote ambaye sio mweusi, utawahesabu kuwa wameibiwa"

Na iwe kama yalivyo maneno yako

Hapa "neno" ina maana ya kitu kilichosemwa. "Itakuwa kana kwamba unasema" au "Tutafanya kile ulichosema"

Genesis 30:35

yaliyokuwa na milia na madoa

"ambazo zilikuwa na milia na madoa"

yaliyokuwa na milia na madoa

"yaliyokuwa na madoa"

kila aliyekuwa mweupe

"kila mbuzi ambaye alikuwa na weupe ndani yake"

na weusi wote katika kondoo,

"na kondoo wote weusi"

akawakabidhi katika mikono

Hapa "mikono" ina maana ya kutawala au kutunza. "akawafanya wanawe kuwatunza"

Genesis 30:37

mipopla .... mlozi ... mwaramoni

Hii yote ni miti ya mbao nyeupe

akatoa maganda ili michilizi myeupe ionekane, na akaifanya sehemu nyeupe ya ndani ya mti iliyokuwa ndani ya fito ionekane

"na kutoa maganda ya mti ili kwamba mbao nyeupe ya chini ionekane"

mabirika yakunyweshe

vyombo virefu vya wazi vinavyoshikilia maji kwa ajili ya wanyama kunywa

Genesis 30:39

Wanyama wakapandana

"Wanyama wa mifugo walizalishana" au "Wanyama walipandana"

wakazaa watoto wenye milia, mabaka na wenye madoa

"wakazaa watoto weney milia na madoa"

Yakobo akawatenga

Inaweza kuwekwa wazi ya kwamba hii ilitokea katika kipindi cha miaka kadhaa. "Katika kipindi cha miaka kadhaa iliyofuata, Yakobo akawagawanya"

kuelekea

"kutazama kuelekea"

kayatenga makundi yake mwenyewe pekee

"aliwatenganisha mifugo wake"

Genesis 30:41

mbele ya macho ya kundi

Hapa "macho" ina maana ya "kuona". "ili kwamba mifugo waweze kuona"

kati ya fito

"mbele ya fito"

wanyama waliodhaifu

"wanyama wenye nguvu chache"

Hivyo wanyama dhaifu wakawa wa Labani, na wenye nguvu wakawa wa Yakobo

"Kwa hiyo wanyama dhaifu wakawa wa Labani, na wale wenye nguvu wakawa wa Yakobo". Unaweza kuiweka wazi zaidi. "Kwa hiyo wanyama dhaifu hawakuwa na milia au madoa na wakawa wa Labani, na wale wenye nguvu hawakuwa na milia au madoa na wakawa wa Yakobo"

Genesis 30:43

Mtu huyo

"Yakobo"

akastawi sana

"akafanikiwa sana" au "akawa tajiri sana"

Genesis 31

Genesis 31:1

Basi

Neno hili linatumika hapa kuweka alama kuweka nafasi katika simulizi kuu. Hapa mwandishi anaanza kueleza sehemu mpya ya simulizi.

Yakobo akasikia maneno ya wana wa Labani, wakisema

Hapa "maneno" yana maana ya kwa yale waliokuwa wakisema. "Yakobo alisikia ya kwamba wana wa Labani wakisema"

Yakobo amechukuwa yote yaliyokuwa ya baba yetu

Wana wa Labani walikuza kwa sababu walikuwa na hasira. "Kila kitu ambacho Yakobo anacho ametoa kwa baba yetu"

Yakobo akaona mwonekano katika uso wa Labani. Akaona kwamba nia yake imebadilika

Sentensi hizi mbili zina maana moja. Ya pili inaelezea muonekano ambao Yakobo aliona kwa uso wa Labani. "Yakobo aligundua ya kwamba Labani hakufurahishwa naye tena"

baba zako

"baba yako Isaka na babu yako Abrahamu"

Genesis 31:4

Yakobo akatuma kuwaita Raheli na Lea uwanjani katika kundi lake la mifugo

"Yakobo akatuma kuwaita Raheli na Lea uwanjani katika kundi lake la mifugo"

katika kundi lake la mifugo naye akawambia

Hii inaweza kuwekwa kama sentensi mbili fupi. "katika mifugo yake. Akawaambia"

Naona nia ya baba yenu kwangu imebadilika

"Nimegundua baba yenu hafurahishwi na mimi tena"

mnajua kwamba ni kwa nguvu zangu zote nimemtumikia baba yenu

Neno "mnajua" hapa lina maana ya wote Raheli na Lea. Pia linaongeza msisitizo. "Nyie wenyewe mnajua ya kwamba nimetumikia baba yenu kwa nguvu zangu zote"

Genesis 31:7

amenidanganya

"amenidanganya" au "hajanitendea haki"

ujira wangu

"alichosema atanilipa"

kunidhuru

Maana zaweza kuwa 1) kudhuru kwa mwili au 2) kusababisha Yakobo ateseke kwa namna yoyote.

Wanyama wenye mabaka

"Wanyama wenye madoa"

kondoo wote walipozaa

"mifugo wakazaa"

wenye milia

"Wanyama wenye milia"

Kwa njia hii Mungu amemnyang'anya mifugo baba yenu na kunipa mimi

"Hivi ndivyo Mungu aliwapatia wanyama wa baba yenu kwangu"

Genesis 31:10

Taarifa ya Jumla

Yakobo anaendelea simulizi yake kwa wake zake Lea na Raheli.

Wakati fulani wa majira ya kupandana

"Wakati wa msimu wa kupandana"

yaliyowapanda kundi

Hapa "kundi" ina maana ya mbuzi wa kike. "kupandana na mbuzi wa kike wa kundi"

yalikuwa ya milia, mabaka na madoa

"walikuwa na milia, madoa kidogo,na mabaka makubwa"

Malaika wa Mungu

Maana zaweza kuwa 1) Mungu mwenyewe alijitokeza kama mtu au 2) mmoja wa wajumbe wa Mungu alijitokeza. Kwa maana msemo haueleweki vizuri, ni vyema kutafsiri kama "malaika wa Mungu" kwa kutumia neno la kawaida linalotumika kwa "malaika".

Nikasema

"Na nikajibu"

Mimi hapa

"Ndio, ninasikiliza" au "Ndio, kuna nini?"

Genesis 31:12

Taarifa ya Jumla:

Malaika wa Bwana anaendelea kuzungumza na Yakobo.

Inua macho yako

Hii ni namna ya kusema "Tazama juu"

wanaolipanda kundi

Hapa "kundi" lina maana ya mbuzi wa kike. "ambao wanawapanda na mbuzi wa kike wa kundi"

Wana milia, madoa na na mabaka

"wana milia na madoa"

mahali ulipoitia nguzo mafuta

Yakobo alimwaga mafuta juu ya nguzo kuiweka wakfu kwa Mungu.

nchi uliyozaliwa

"nchi ambayo ulizaliwa"

Genesis 31:14

Raheli na Lea wakajibu na kumwambia

Hii haimaanishi walizungumza katika wakati mmoja. Inasisitiza ya kwamba walikubaliana wao kwa wao.

Je kuna sehemu yoyote au urithi wetu katika nyumba ya baba yetu?

Raheli na Lea wanatumia swali kusisitiza ya kwamba hakuna kitu kilichosalia kutoka kwa baba yao kuwapatia. "Hakuna kitu chochote kabisa kilichobaki kwa ajili yetu kurithi kutoka kwa baba yetu!"

Je hatutendei kama wageni?

Wanatumia swali kuonyesha hasira yao kuhusu jinsi baba yao anavyowatendea. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Baba yetu anatutendea kama wanawake wageni badala ya binti zake!"

Kwa maana ametuuza na kwa ujumla ametapanya pesa zetu. 16Mali zote

Hii inaweza kuwekwa kwa uwazi zaidi. "Ametuuza kwa manufaa yake mwenyewe"

na kwa ujumla ametapanya pesa zetu

Labani kutumia fedha yote ambayo alipaswa kuwapatia binti zake inazungumziwa kana kwamba alikuwa mnyama pori aliyekula fedha yote kana kwamba ilikuwa chakula. "alitumia fedha yetu yote"

na sasa ni zetu na watoto wetu

"inakuwa ya kwetu na watoto wetu"

Sasa basi

Hapa "sasa" haimaanishi "katika kipindi hiki" lakini inatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.

lolote Mungu alilokuambia, fanya

"fanya yote ambayo Mungu alikuambia kufanya"

Genesis 31:17

wanawe

Yakobo aliwachukua watoto wake wote. Inataja watoto wa kiume pekee kwa sababu walikuwa muhimu kama warithi wake.

Akawaongoza mifugo wake wote

"Akawaongoza mifugo wake wote" Hapa "mifugo" ina maana ya wanyama wake wote wa kufuga.

wakiwemo wanyama aliowapata huko Padani Aramu

"wakiwemo mifugo wengine ambao aliwachukua umiliki alipokuwa Padani Aramu"

Kisha akaenda kuelekea kwa Isaka baba yake katika nchi ya Kanaani

"Alienda katika nchi ya Kaanani, ambapo Isaka baba yake alikuwa akiishi"

Genesis 31:19

Labani alipokuwa amekwenda kuwakata manyoya kondoo wake

"Wakati Labani alipoondoka kukata manyoya ya kondoo"

mto

Hii ina maana ya mto wa Frati.

akaenda kuelekea

"kusafiri kuelekea"

vilima ya Gileadi

"milima ya Gileadi" au "Mlima Gileadi"

Genesis 31:22

Labani akaambiwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "mtu mmoja akamwambia Labani"

Siku ya tatu

Ilikuwa utamaduni wa Kiyahudi kuhesabu siku ya kuanza safari kama siku ya kwanza. "Siku mbili baada ya kuondoka"

kwamba Yakobo amekimbia

Yakobo pekee ndiye anayetajwa kwa sababu ndiye kiongozi wa familia. Inaweza kuwekwa wazi ya kwamba familia yake ilikwenda naye. "ya kwamba Yakobo alitoroka na wake zake na watoto wake"

Hivyo akawachukua

"Kwa hiyo labani akachukua"

na kumfuatia

"na kumfukuza Yakobo"

kwa safari ya siku saba

Labani alitumia siku saba akitembea kumfikia Yakobo.

Akampita

"Alimfikia"

Genesis 31:24

Basi Mungu akaja kwa Labani Mwarami katika ndoto usiku

Neno "basi" linatumika kuweka alama kwa badiliko kutoka kwenye simulizi ya taarifa ya nyuma kuhusu Labani. "usiku huo Mungu alikuja kwa Labani ndotoni"

Ujiadhari kumwambia Yakobo jambo lolote liwe jema au baya

Msemo huu "jema au baya" unatumika pamoja kumaanisha "chochote". "Usiseme chochote kujaribu kumsimamisha Yakobo kuondoka"

Labani akampata Yakobo. Basi Yakobo alikuwa amepiga hema yake katika nchi ya vilima. Labani pia akapiga kambi pamoja na ndugu zake katika nchi ya kilima ya Gileadi

Neno "basi" inatumika hapa kuweka alama ya badiliko ya simulizi kwa taarifa ya nyuma kuhusu Yakobo na Labani. "Labani alipomfikia Yakobo, Yakobo aliweka hema lake katika nchi ya vilima. Kisha Labani na ndugu zake pia waliweka mahema katika nchi ya Gileadi.

Genesis 31:26

umewachukua binti zangu kama mateka wa vita

Labani anamzungumzia Yakobo kuchukua familia yake pamoja naye mpaka katika nchi ya Kaanani kana kwamba Yakobo aliwachukua mateka baada ya vita na anawalazimisha wao kuondoka nao. Labani anatia chumvi kwa sababu ana hasira na anajaribu kumfanya Yakobo asikie hatia kwa kile alichokifanya.

umekimbia kwa siri

"kukimbia kwa siri"

kwa sherehe

"kwa furaha"

kwa matari na vinubi

Vyombo hivi ni vya muziki. "na kwa muziki"

matari

chombo cha muziki chenye kichwa kama ngoma ambacho kinapigwa na kina vipande vya chuma kimekizunguka pembeni vyenye sauti pale chombo kikitikiswa.

niwabusu wajukuu wangu

Hapa "wajukuu" wanajumlisha wajukuu wote wakiume na kike. "kubusu wajukuu wangu"

Basi umefanya upumbavu

"umefanya upumbavu"

Basi

Hapa haimaanishi "katika kipindi hiki" lakini inatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.

Genesis 31:29

Iko katika uwezo wangu kukudhuru

Neno "kukudhuru" ni wingi na una maana ya kila mmoja aliyekuwa na Yakobo. "Nina watu wa kutosha pamoja nami kuwadhuru nyote"

Jiadhari usimwambie Yakobo neno la heri wala shari

Maneno "heri au shari" yanatumika pamoja kumaanisha "chochote". "Usiseme chochote kujaribu kumzuia Yakobo kuondoka"

umeondoka

Hapa "umeondoka" ni umoja na ina maana ya Yakobo.

nyumba ya baba yako

Hapa "nyumba" ina maana ya familia. "kuwa nyumbani na baba yako na familia yako yote"

miungu yangu

"sanamu zangu"

Genesis 31:31

kwa sababu niliogopa na kudhani kuwa ungeninyang'anya binti zako kwa nguvu ndiyo maana nikaondoka kwa siri

"Niliondoka kwa siri kwa sababu niliogopa ya kwamba ungewachukua binti zako kutoka kwangu kwa lazima"

Yeyote aliyeiiba miungu yako hataendelea kuishi

Hii inaweza kuwekwa katika hali ya chanya. "Tutamuua yeyote aliyechukua miungu yako"

Mbele ya ndugu zetu

Neno "zetu" lina maana ya ndugu wa Yakobo na inajumuisha ndugu za Labani. Ndugu wote watatazama kuhakikisha kila kitu ni cha haki na kweli.

onesha chochote kilichochako nilichonacho na uchukue

"tafuta chochote tulichonacho ambacho ni chako na uchukue"

Kwa maana Yakobo hakujua kwamba Raheli alikuwa ameviiba

Hii inabadilisha kutoka kwa simulizi kwenda kwa taarifa ya nyuma kuhusu Yakobo.

Genesis 31:33

wajakazi wawili

Hii ina maana ya Zilfa ba Bilha.

hakuviona

"hakupata sanamu zake"

Genesis 31:34

Basi Raheli ... juu yake

Neno "basi" linatumika hapa kuweka alama ya badiliko kutoka kwa simulizi kwenda kwa taarifa ya nyuma kuhusu Raheli.

tandiko

kiti kinachowekwa mgongoni mwa mnyama ili mtu aweze kukaa juu yake.

bwana wangu

Kumuita mtu "bwana wangu" ni njia ya kumheshimu.

siwezi kusimama mbele yako

"kwa sababu siwezi kusimama mbele zako"

kwani nipo katika kipindi changu

Hii ina maana ya kipindi cha mwezi ambapo mwanamke hutokwa na damu kutoka kwenye uzazi wake.

Genesis 31:36

Akamwambia

"Yakobo alimwambia Labani"

Kosa langu ni nini? Dhambi yangu ni ipi, hata ukanifuatia kwa ukali?

Misemo ya "Kosa langu ni nini" na "Dhambi yangu ni ipi" zina maana moja. Yakobo anamuuliza Labani amwambie ni kipi alichokosea. "Kosa langu ni lipi mpaka unifuate namna hii?"

ukanifuatia kwa ukali

Hapa neno la "ukali" ina maana ya Labani kumfukuza kwa haraka kwa lengo la kumkamata.

Umeona nini kati ya kitu chochote cha nyumbani mwako

"Umepata nini ambacho ni cha kwako?"

Viweke hapa mbele ya ndugu zetu

Hapa neno "zetu" ina maana ya ndugu wa Yakobo na inajumuisha ndugu wa Labani. "Laza chochote ulichokuta mbele ya ndugu zetu"

waamue kati yetu wawili

Hapa "yetu wawili" ina maana ya Yakobo na Labani. Msemo "waamue kati" ina maana ya kuamua mtu yupi yupo sahihi katika ugomvi huu. "wanaweza kuhukumu kati yetu"

Genesis 31:38

Taarifa ya Jumla:

Yakobo anaendelea kuzungumza na Labani.

miaka ishirini

"miaka 20"

Kondoo

kondoo wa kike

hawakutoa mimba

Hii ina maana ya kwamba hawajawa na mimba iliyokatishwa mapema na bila matarajio na mwanakondoo au mbuzi kuzaliwa amekufa.

Kilichoraruliwa na mnyama sikukuletea

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mnyama pori alipowaua mmoja wa wanyama wako sikukuletea kwako"

Badala yake, nilichukua upotevu huo

Kwa Yakobo kuhesabu wanyama wa Labani waliokufa kama hasara kutoka kwa mifugo wake inazungumzwa kana kwamba ilikuwa mzigo ambao angeubeba begani mwake. "badala ya kuhesabu hasara kutoka kwa mifugo yako, nimehesabu kama hasara kutoka kwa mifugo yangu"

Nilikuwepo wakati wote; mchana joto lilinipata, na baridi wakati wa usiku

Kuteseka wakati wa jua kali na halijoto chini inazungumzwa kana kwamba halijoto ilikuwa wanyama waliokuwa wakimla Yakobo. "Nilikaa na mifugo wako hata wakati wa joto kali la siku na wakati wa baridi wa usiku"

Genesis 31:41

Taarifa ya Jumla

Yakobo anaendelea kuzungumza na Labani.

Miaka hii ishirini

"Miaka hii 20 iliyopita"

miaka kumi na nne

"miaka 14"

Umebadili ujira wangu mara kumi

"amebadili kile alichosema angenilipa mara kumi"

Isipokuwa Mungu wa baba yangu, Mungu wa Ibrahimu, yule Isaka anayemwofu, amekuwa nami

Yakobo ana maana ya Mungu yule yule na sio kwa miungu watatu tofauti. "Kama Mungu wa Abrahamu, na Isaka, baba yangu, asingekuwa na mimi"

Mungu wa baba yangu

Hapa neno "baba" lina maana ya mzazi wake, Isaka.

yule Isaka anayemwofu

Hapa neno "anayemwofu" lina maana ya "hofu ya Yahwe" ambayo ina maana ya kumheshimu kwa ndani na kuonyesha heshima hiyo kwa kumtii yeye.

mikono mitupu

mikono Hii ina maana kutokuwa na kitu. "bila kitu chochote"

Mungu ameliona teso langu na jinsi nilivyofanya kazi kwa bidii

Nomino inayojitegemea "teso" inaweza kuwekwa kama "kuteswa". "Mungu ameona jinsi nilivyofanya kazi kwa bidii na jinsi ulivyonitesa"

Genesis 31:43

akini nitafanya nini leo kwa hawa binti zangu, au kwa watoto wao waliowazaa?

Labani anatumia swali kusisitiza ya kwamba hakuna awezalo kufanya. Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Lakini hakuna kitu nachoweza kufanya kuwarudisha binti zangu na wajukuu wangu kwangu"

liwe shahidi

Hapa neno "shahidi" haimaanishi mtu, lakini linatumika kwa mfano na lina maana ya agano ambalo Yakobo na Labani walifanya. Agano linazungumzwa kana kwamba lilikuwa mtu ambaye alikuwa pale wakati walipokubaliana kufanya amani kati yao.

Genesis 31:45

nguzo

Hii ina maana ya kwamba jiwe kubwa liliwekwa mwishoni pake kuweka alama ya sehemu ambapo tukio hili la muhimu lilitokea.

kufanya rundo

"kuzipangilia juu ya nyenzake"

Kisha wakala pale kati ya lile rundo

Kula chakula pamoja ilikuwa sehemu ya kufanya agano baina yao. Maana kamili ya hii inaweza kuwekwa wazi.

Yega Saha Dutha

"Jina la Yega Saha Dutha lina maana ya "fungu la mashahidi" kwa lugha ya Labani.

Galedi

"Jina la Galedi lina maana ya "fungu la mashahidi" kwa lugha ya Yakobo.

Genesis 31:48

Rundo hili ni shahidi kati yangu nawe leo

Mawe hayawi mashahidi halisi kwa ajili ya mtu. "Rundo hili litakuwa ukumbusho kati yangu na wewe"

Galedi

"Jina la Galedi lina maana ya "fungu la mashahidi" kwa lugha ya Yakobo.

Mispa

"Jina la Mispa lina maana ya "mnara".

tunapokuwa hatuonani

Hapa "nje ya macho" ina maana ya kutokuwa machoni pa mwenzako. "tutakapokuwa hatupo machoni mwetu sisi wawili"

japokuwa hakuna mwingine yupo nasi

Hapa "nasi" ina maana ya Labani na Yakobo. "hata kama hakuna mtu wa kutuona"

tazama

"kumbuka". Hii inaongeza msisitizo kwa kile kinachosemwa baadae.

Genesis 31:51

Rundo hili ni shahidi

Marundo haya ya mawe yalikuwa tendo ya kumbukumbu na alama ya mpaka kwa Yakobo na Labani kuhusu makubaliano yao ya amani. Yanazungumzwa kana kwamba ni mashahidi kama watu.

Mungu wa Ibrahimu, na mungu wa Nahori, miungu ya baba zao, waamue kati yetu

Abrahamu ni babu yake Yakobo. Nahori ni babu yake Labani. Baba wa Abrahamu na Nahori ni Tera. Sio wote walimuabudu Yahwe.

Hofu ya Isaka baba yake

Hapa neno "Hofu" lina maana ya Yahwe, ambaye Isaka alimheshimu kwa ndani na kuonyesha heshima hiyo kwa kumtii yeye.

Genesis 31:54

akawaita ndugu zake kula chakula

Kula chakula pamoja ilikuwa sehemu ya kufanya agano baina na mtu. Maana kamili ya hii inaweza kuwekwa wazi.

asubuhi na mapema ... kurudi kwake

Mstari wa 55 ni mstari wa kwanza wa sura ya 32 katika maandishi ya asili ya Kihebrania, lakini mstari wa mwisho wa suraya 31 katika Biblia za sasa. Tunashauri kufuata hesabu ya Biblia ya lugha yako.

kuwabariki

Hii ina maana ya kuweka nia kwa mambo chanya na yenye manufaa yanayotokea kwa mtu.

Genesis 32

Genesis 32:1

Mahanaimu

"Jina la Mahanaimu lina maana ya "kambi mbili"

Genesis 32:3

Seiri

Hili ni eneo lenye milima katika eneo la Edomu.

Hivi ndivyo mtakavyosema kwa bwana wangu Esau: Hivi ndivyo mtumishi wako Yakobo asemavyo: 'Nimekuwa ... mbele zako

Hii ina nukuu ndani ya nukuu. Nukuu ya moja kwa moja inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Hivi ndivyo nataka ukamwambie bwana wangu Esau. Mwambie nimekuwa ... machoni pake."

bwana wangu Esau

Yakobo anatumia lugha ya upole na anamtaja kaka yake kama "bwana wangu".

mtumishi wakoYakobo

Yakobo anatumia lugha ya upole na anajiita mwenyewe kama "mtumishi wako".

ili kwamba nipate kibali mbele zako.

Hapa "machoni" ina maana ya fikra na mawazo ya mtu. "ili kwamba unithibitishe"

Genesis 32:6

watu mia nne

"wanamume 400"

alipoogopa

HIi ina maana ya hisia zisizo nzuri ambazo mtu anazo pale anapopata tishio la kudhuriwa kwake au wengine.

kutaabika

"tia wasiwasi" au "kutaabishwa"

kambi moja, ndipo kambi nyingine itakaposalimika

Hapa "kambi" ina maana ya watu. "kuwashambulia watu katika kambi moja, kisha watu wa kambi nyingine watatoroka"

Genesis 32:9

Mungu wa baba yangu Ibrahimu, na Mungu wa baba yangu Isaka, Yahwe

Hii haimanishi mungu wawili, lakini kwa Mungu mmoja wanaomuabudu wote. "Yahwe, ambaye ni Mungu wa babu yangu Abrahamu na baba yangu Isaka"

Yahwe, aliyeniambia, 'Rudi katika nchi yako na kwa jamaa yako, nami nitakustawisha

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isyo moja kwa moja. "Yahwe, wewe uliyesema ya kwamba nirudi katika nchi na kwa jamaa yangu, na kwamab utanifanikisha"

na kwa jamaa yako

"na kwa familia yako"

nitakustawisha

"Nitafanya mema kwako" au "Nitakutendea mema"

Mimi sistahili matendo yako yote ya agano la uaminifu na ustahilifu wote uliomfanyia mtumishi wako

Nomino zinazojitegemea "uaminifu" na "mkweli" inaweza kuwekwa kama "mwaminifu". "Sistahili wewe uwe mwaminifu kwa agano lako au kwako kuwa mwaminifu kwangu, mtumishi wako"

mtumishi wako

Hii ni njia ya upole ya kusema "mimi"

sasa nimekuwa matuo mawili

Hapa "nimekuwa" inamaana ya kile ambacho anacho sasa. "na sasa nina watu wa kutosha, mifugo, na mali kutengeneza kambi mbili"

Genesis 32:11

niokoe

"niokoe"

kutoka katika mikono ya ndugu yangu, mikono ya Esau

Hapa neno "mikono" ina maana ya nguvu. Misemo miwili ina maana moja. Msemo wa pili unaelezea ya kwamba kaka ambaye Yakobo alikusudia ni Esau. "kutoka kwa nguvu ya kaka yangu, Esau" au "kutoka kwa kaka yangu, Esau"

namwogopa, kwamba

"Ninaogopa ya kwamba"

Lakini ulisema, 'hakika nitakufanya ufanikiwe. Nitaufanya uzao wako ... hesabu.'

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Lakini ulisema ya kwamba utanitafanikisha, na kwamba utafanya uzao wangu .. hesabu"

nitakufanya ufanikiwe

"kufanya mema kwako" au "kukutendea mema"

Nitaufanya uzao wako kuwa kama mchanga wa bahari

Hii inazungumzia hesabu kubwa ya uzao wa yakobo kana kwamba hesabu yake itakuwa kama chembe za mchanga za pwani za baharini.

ambao hauwezi kuhesabika kwa hesabu yake

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ambayo hakuna mtu awezaye kuhesabu kwa sababu ya hesabu yake"

Genesis 32:13

mia mbili

"200"

ishirini ... thelathini ... arobaini ... kumi

"20 ... 30 ... 40 ... 10"

na wana wao

"na watoto wao"

Akawaweka katika mikono ya watumishi wake, kila kundi peke yake.

Hapa "katika mikono" ina maana ya kutoa mamlaka juu yao. "Aliwagawa katika makundi madogo, na kuwapa kila mmoja wa watumishi wake mamlaka juu ya makundi"

mwache nafasi kati ya makundi ya wanyama

"na kila kundi lisafiri kwa umbali kutoka kwa kundi lingine"

Genesis 32:17

Akamwagiza

"Akamuamuru"

kukuuliza .... ambao wako mbele yenu?

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "kukuuliza bwana wako ni nani, unakwenda wapi, na nani anamiliki wanyama walio mbele yako"

ni wa nani?

"Bwana wako ni nani?"

wanyama hawa mbele yenu ni wa nani?

"Nani anamiliki wanyama hawa ambao wako mbele yako?"

Ndipo umwambie, 'Ni wa mtumishi wako Yakobo. Ni zawadi wanaopelekwa kwa bwana wangu Esau. Na tazama, yeye pia anakuja nyuma yetu."

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Kisha ntataka kumwambia ya kwamba vitu vyote hivi ni vya Yakobo, mtumishi wake, na anampatia bwana wake, Esau. Na mwambie ya kwamba Yakobo yupo njiani kukutana naye"

mtumishi wako Yakobo

Yakobo anajifafanua kwa njia ya upole kama mtumishi wa Esau.

kwa bwana wangu Esau

Yakobo anajifafanua kwa Esau kwa njia ya upole kama bwana wake.

anakuja nyuma yetu

Hapa "yetu" ina maana ya mtumishi akizungumza na watumishi wengine kuleta mifugo kwa Esau.

Genesis 32:19

akatoa maelekezo kwa kundi la pili

"akaamuru kundi la pili"

Mnapaswa pia kusema, 'mtumwa wako Yakobo

Maana zaweza kuwa 1) "Utasema pia, 'Mtumishi wako Yakobo"' au 2) 'Utasema, "Pia, Mtumishi wako Yakobo"'.

nitamtuliza

"Nitamtuliza" au "Nitafanya hasira yake itoweke"

atanipokea

"atanikaribisha kwa upole"

Hivyo zawadi zikatangulia mbele yake

Hapa "zawadi" ina maana ya watumishi kupeleka zawadi zile.

Yeye mwenyewe akakaa

Hapa "mwenyewe" inasisitiza ya kwamba yakobo hakuwenda pamoja na watumishi wake.

Genesis 32:22

wajakazi wake wawili

"watumishi wake wawili wake zake". Hii ina maana ya Zilpa na Bilha.

kijito

sehemu ya kina kifupi ya mto ambayo ni rahisi kuvuka.

Yaboki

Hili ni jina la mto.

mali yake yote

"kila kitu alichokuwa nacho"

Genesis 32:24

mpaka alfajiri

"mpaka alfajiri"

nyonga

"kiungo cha paja". Hii ni sehemu ambapo mfupa wa juu wa mguu unaungana na nyonga.

Nyonga ya Yakobo ikatenguka alipokuwa akishindana naye

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mwanamume alijeruhi nyonga ya Yakobo aliposhindana naye"

kwani kunakucha

"jua litachomoza hivi karibuni"

umenibariki

Hapa "umenibariki" ina maana ya kutamka baraka maalumu juu ya mtu na kusababisha mambo mazuri kutokea kwa huyo mtu.

sitakuacha uende mpaka uwe umenibariki

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya chanya. "Haiwezekani! Lazima unibariki kwanza, ndipo nitakuacha uondoke"

Genesis 32:27

Israeli

"Jina la Israeli lina maana ya 'Anayeshindana na Mungu'"

na wanadamu

Hapa "wanadamu" ina maana ya "watu" kwa ujumla.

Genesis 32:29

Akasema, "Kwa nini kuniuliza jina langu?"

Akasema, "Kwa nini kuniuliza jina langu?" Swali hili la balagha lilitakiwa kushtua, kukaripia na kumfanya Yakobo awaze juu ya kilichotokea kati yake na mtu mwingine aliyeshindana naye. "Usiniulize jina langu!"

Penieli

"Jina la Penieli lina maana ya "uso wa Mungu".

uso kwa uso

Kuwa "uso kwa uso" ina maana ya watu wawili kutazamana ana kwa ana, kwa umbali mfupi.

na maisha yangu yamesalimika

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "na bado akasalimisha maisha yangu"

Genesis 32:31

Ndiyo maana wana hadi siku ya leo

Hii inafanya mabadiliko kutoka kwa simulizi kwenda kwa taarifa ya nyuma kuhusu vizazi vya Israeli.

hadi siku ya leo

Hii ina maana siku ambayo mwandishi alikuwa akiandika hivi.

kano za nyonga

Hii ina maana ya msuri unaonganisha mfupa wa paja na kiungo cha paja.

kiungo cha nyonga

"kiungo cha paja"

alipotegua

"alipokuwa akipiga"

Genesis 33

Genesis 33:1

tazama

Neno "tazama" hapa linatuamsha kuvuta nadhari juu ya sehemu mpya ya simulizi ya kushangaza.

watu mia nne

"wanamume 400"

Yakobo akawagawanya watoto ... wajakazi wawili wakike

Hii haimaanishi Yakobo aliwagawanya watoto wake sawa sawa ili kwamba kila mwanamke awe na idadi sawa ya watoto pamoja nao. Yakobo aliwagawa watoto ili kila mmoja aondoke na mama yake.

watumishi wa kike

"watumishi wa kike wake zake". Hii ina maana ya Bilha na Zilpa"

Yeye mwenyewe akatangulia mbele yao

Hapa "mwenyewe" inasisitiza ya kwamba Yakobo aliondoka peke yake mbele ya wenzake.

Akasujudu

Hapa neno "sujudu" lina maana ya kuinama chini kuonyesha kwa unyenyekevu heshima na taadhima kwa mtu.

Genesis 33:4

kumlaki

"kukutana na Yakobo"

akamkumbatia, akakumbatia shingo yake na kumbusu

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. "Esau aliweka mikono yake kumzunguka Yakobo, kumkumbatia, na kumbusu"

Kisha wakalia

Hii inaweza kusemwa kwa uwazi zaidi. "Kisha Esau na Yakobo wakalia kwa sababu walikuwa na furaha kuonana tena"

aliona wanawake na watoto

"akawaona wanawake na watoto waliokuwa na Yakobo"

Ni watoto ambao Mungu amempa mtumishi wako

Msemo "mtumishi wako" ni njia ya upole ya Yakobo akimaanisha yeye mwenyewe. "Hawa ni watoto ambao Mungu amenipatia mtumishi wako, kwa neema yake"

Genesis 33:6

watumishi wa kike

"watumishi wa kike wake zake". Hii ina maana ya Bilha na Zilpa.

wakasujudia

Hii ni ishara ya unyenyekevu na heshima mbele za mtu mwingine.

Unamaanisha nini kwa makundi haya yote niliyokutana nayo?

Msemo wa "makundi haya yote" una maana ya makundi ya watumishi ambao Yakobo aliwatuma kutoa zawadi kwa Esau. "Kwa nini ulituma makundi haya yote tofauti kuja kukutana nami?"

Kutafuta kibali machoni mwa bwana wangu.

Hapa "machoni" ina maana ya fikra na mawazo ya mtu. "Ili kwamba wewe, bwana wangu, ufurahishwe na mimi"

bwana wangu

Msemo "bwana wangu" ni njia ya upole inayomaanisha Esau.

Genesis 33:9

Ninayo ya kutosha

Neno "wanyama" au "mali" linaeleweka. "Nina wanyama wa kutosha" au "Nina mali ya kutosha"

ikiwa nimeona kibali machoni pako

Hapa "machoni" ina maana ya fikra au mawazo ya mtu. "Kama unapendezwa na mimi"

zawadi yangu kutoka mkononi mwangu

Hapa "mkononi" ina maana ya Yakobo. "zawadi hii nayokupatia"

mkononi mwangu, kwa maana

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. "mkono wangu. Kwa uhakika"

nimeona uso wako, na ni kama kuona uso wa Mungu

Maana ya tashbihi hii haipo wazi. Maana zaweza kuwa 1) Yakobo amefurahi ya kwamba Esau amemsamehe kama Mungu alivyomsamehe au 2) Yakobo anashangazwa kumuona kaka yake tena kama alivyoshangazwa kumuona Mungu au 3) Yakobo ananyenyekea kuwa mbele ya Esau kama alivyonyenyekea kuwa mbele za Mungu.

nimeona uso wako

Hapa "uso" ina maana ya Esau. Ni vyema kutafsiri kama "uso" kwa sababu ya umuhimu wa neno "uso" hapa pamoja na "uso wa Mungu" na "uso kwa uso" katika 32:29.

uliyoletewa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ambazo watumishi wangu wamekuletea"

Mungu amenitendea kwa neema

"Mungu amenitendea wema sana" au "Mungu amenibariki sana"

Hivyo Yakobo akamsihi, na Esau akamkubali

Ilikuwa utamaduni kukataa zawadi kwanza, lakini kukubali zawadi ile baadae kabla ya mtoaji kukwazika.

Genesis 33:12

Bwana wangu anajua

Hii ni njia ya upole na maalumu ya kumhusu Esau. "Wewe, bwana wangu, unajua"

watoto ni wadogo

Maana inaweza kuwekwa wazi zaidi. "watoto ni wadogo sana kusafiri haraka"

Ikiwa watapelekwa kwa haraka hata siku moj

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "tukiwalazimisha kwenda haraka sana hata kwa siku moja"

Tafadhari bwana wangu na amtangulie mtumishi wake

Hii ni njia ya upole na maalumu ya Yakobo kujitaja mwenyewe. "Bwana wangu, mimi ni mtumishi wako. Tafadhali nenda mbele yangu"

kwa kadili ya mifugo iliyo mbele yangu

"kwa kasi ya wanyama naowatunza wanaweza kwenda"

Seiri

Hili ni eneo lenye milima katika eneo la Edomu.

Genesis 33:15

Kwa nini kufanya hivyo?

Yakobo anatumia swali kuweka msisitizo ya kwamba Esau hahitaji kubakiza wanamume. "Usifanye hivyo!" au "Hahitaji kufanya hivyo!"

Bwana wangu amekuwa

Hii ni njia ya upole na maalumu ya kumaanisha Esau. "Wewe, bwana wangu, umekuwa"

Sukothi

"Jina la Sukothi lina maana ya "hifadhi".

akajijengea nyumba

Inasemekana ya kwamba nyumba ni ya familia yake pia. "alijenga nyumba kwa ajili yake mwenyewe na familia yake"

kwa ajili ya mifugo wake

"kwa wanyama aliowatunza"

Genesis 33:18

Taarifa ya Jumla:

Hii inaanza sehemu mpya ya simulizi. Mwandishi anaelezea kile Yakobo alichofanya baada ya kupumzika Sukothi.

Yakobo alipokuja kutoka Padani Aramu

"Baada ya Yakobo kuondoka Padani Aramu"

Yakobo ... alipokuja ... Akapiga kambi

Hii inamtaja Yakobo pekee kwa sababu ni kiongozi wa familia. Inasemekana ya kwamba familia yake ilikuwa pamoja naye.

Akapiga kambi karibu

"Aliweka kambi yake karibu"

sehemu ya ardhi

"kipande cha ardhi"

Hamori

Hili ni jina la mwanamume.

baba wa Shekemu

Shekemu ni jina la mji na jina la mwanamume.

mia

"100"

El Elohe Israeli

"Jina la El Elohe Israeli lina maana ya "Mungu, Mungu wa Israeli"

Genesis 34

Genesis 34:1

Basi

Hapa neno hili linatumika kuweka alama kwa sehemu mpya ya simulizi.

Dina

Hili ni jina la binti wa Lea.

Mhivi

Hili li jina la kundi la watu.

mwana wa mfalme wa nchi

Hii ina maana ya Hamori na sio Shekemu. Pia "mwana wa mfalme" hapa haimaanishi mtoto wa mfalme. Ina maana ya Hamori alikuwa kiongozi wa watu katika eneo hilo.

akamkamata kwa nguvu na kulala naye

Shekemu alimbaka Dina.

Akavutiwa na Dina

"Alivutiwa sana na yeye". Hii inazungumzia juu ya Shekemu kumpenda Dina na kutaka kuwa naye kana kwamba kuna jambo lililokuwa likimlazimisha kwenda kwa Dina. Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "Alitaka sana kuwa na Dina"

kuongea naye kwa upole

Hii ina maana aliongea naye kwa upole kumuaminisha ya kwamba alimpenda na kwamba alimtaka pia ampende yeye.

Genesis 34:4

Basi Yakobo

"basi" inatumika hapa kuweka alama ya badiliko kutoka kwa simulizi kwenda kwa taarifa ya nyuma kuhusu Yakobo.

Yakobo akasikia kwamba alikuwa

Neno "alikuwa" lina maana ya Shekemu

alikuwa amemchafua

Hii ina maana ya kwamba Shekemu alivunja sana heshima na kumuabisha Dina kwa kumlazimisha alale naye.

akawangoja

Hii ni namna ya kusema ya kwamba Yakobo hakusema au kufanya jambo kuhusu suala hili.

Genesis 34:6

Hamori ... akaenda kuongea na Yakobo

"Hamori ... akaenda kuongea na Yakobo"

Watu hawa walichukizwa

"Wanamume walikasirika"

Walikasirika sana ... halikupasa kutendeka

Hii inaweza kuwekwa kama nukuu ya moja kwa moja iliyozungumzwa na wana wa Yakobo.

amemwaibisha Israeli

Hapa neno la "Israeli" lina maana ya kila mtu katika familia ya Yakobo. Israeli kama kundi la watu liliabishwa."ameabisha familia ya Israeli" au "ameleta aibu juu ya watu wa Israeli"

kumlazimisha binti wa Yakobo

"kumvamia binti wa Yakobo"

kwa maana jambo kama hilo halikupasa kutendeka

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "kwa maana hakupaswa kufanya jambo baya kama hilo"

Genesis 34:8

Hamori akaongea nao

"Hamori alizungumza na Yakobo na wanawe"

anampenda binti yenu

Hapa neno "anampenda" lina maana ya upendo wa kimahaba kati ya mwanamume na mwanamke. "anampenda na anataka kumuoa"

mpeni kuwa mke wake

Katika baadhi ya tamaduni, wazazi huamua watoto wao wataolewa na nani"

Mwoane nasi

Kuoana ni kuoa mtu wa jamii, kabila, au dini tofauti. "Ruhusu ndoa kati ya watu wako na wetu"

nchi itakuwa wazi kwa ajili yenu

"nchi itakuwa wazi kwako"

Genesis 34:11

Shekemu akamwambia baba yake

"Shekemu alimwambia baba yake Dina Yakobo"

Na nione kibari machoni penu, na chochote mtakachoniambia nitatoa

Hapa "machoni" ina maana ya fikra na mawazo ya mtu. "Kama utanipa kibali, basi nitakupa chochote utakachokiomba"

mahari

Katika baadhi ya tamaduni, ni kawaida kwa mwanamume kutoa fedha, mali, ng'ombe, na zawadi zingine kwa familia ya mwanamke katika kipindi cha ndoa.

Wana wa Yakobo wakamjibu Shekemu na Hamori baba yake kwa hila

Nomino inayojitegemea ya "hila" inaweza kuwekwa kama kitenzi cha "kudanganya". "Lakini wana wa Yakobo walimdanganya Shekemu na Hamori walipowajibu"

Shekemu alikuwa amemnajisi Dina

Hii ina maana ya kwamba Shekemu aliwavunjia heshima sana na kumuabisha Dina kwa kumlazimisha kulala naye.

Genesis 34:14

Wakawambia

"wana wa Yakobo waliwaambia Shekemu na Hamori"

Hatuwezi kufanya jambo hili, kumpa dada yetu

"Hatuwezi kukubali kumtoa Dina katika ndoa"

kwani hiyo ni aibu kwetu

"kwa maana hiyo itasababisha aibu kwetu". Hapa "kwetu" ina maana ya wana wa Yakobo na watu wote wa Israeli.

tutakapowapa binti zetu ... tutachukua binti zenu kwetu sisi wenyewe

Hii ina maana wataruhusu mtu kutoka familia ya Yakobo kuoa mtu anayeishi katika nchi ya Hamori.

Genesis 34:18

Maneno yao yakawafurahisha Hamori na Shekemu mwanaye

Hapa "maneno" ina maana ya kile kilichosemwa. "Hamori na mwanawe Shekemu walikubali na kile ambacho wana wa Yakobo walisema"

kufanya walichokisema

"kufanyiwa tohara"

binti wa Yakobo

"binti wa Yakobo Dina"

kwa sababu alikuwa mtu aliyeheshimiwa sana katika nyumba ya babaye

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. Inaweza kuwekwa wazi ya kwamba Shekemu alijua wanamume wengine wangekubali kufanyiwa tohara kwa sababu walimheshimu sana. "Shekemu alijua wanamume wote katika nyumba ya baba yake watakubaliana naye kwa sababu alikuwa akiheshimiwa zaidi kati yao"

Genesis 34:20

lango la mji wao

Ilikuwa kawaida kwa viongozi kukutana katika lango la mji kufanya maamuzi rasmi.

Watu hawa

"Yakobo, wanawe, na watu wa Israeli"

wana amani nasi

Hapa "nasi" inajumlisha Hamori, mwanawe na watu wote waliozungumza nao langoni mwa mji.

waishi katika nchi na kufanya biashara humo

"waruhusu waishi na kufanya biashara katika nchi"

maana, kweli, nchi ni kubwa ya kuwatosha

Shekemu anatumia neno "kweli" kuongeza msisitizo kwa kauli yake. "kwa sababu, hakika, nchi ni kubwa ya kutosha kwa ajili yao" au "kwa sababu, haswa, kuna nchi ya kutosha kwa ajili yao"

tuwachukue binti zao ... tuwape binti zetu.

Hii ina maana ya ndoa kati ya wanawake wa kundi moja na wanamume wa kundi lingine.

Genesis 34:22

Taarifa ya Jumla:

Hamori na Shekemu mwanawe wanaendelea kuzungumza na viongozi wa mji.

Kwa sharti hili pekee watu hawa wanakubali kuishi nasi na kuwa wamoja: ikiwa kila mwanamme miongoni mwetu atatahiriwa, kama wao.

"Kwa sharti hili pekee iwapo kila mwanamume kati yetu atafanyiwa tohara, kama wanamume wa Israeli walivyotahiriwa, ndipo watakubali kusihi miongoni mwetu na kujiunga nasi kama kundi moja"

Je wanyama wao na vitu vyao - wanyama wao wote kuwa wetu?

Shekemu anatumia swali kusisitiza ya kwamba mifugo wa Yakobo na mali zitakuwa za watu wa Shekemu. Hii inaweza kutafsiriwa kama kauli. "Wanyama wao wote na mali zitakuwa zetu"

Genesis 34:24

Kila mwanamme alifanyiwa tohara

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Kwa hiyo Hamori na Shekemu wakawa na mtu wa kufanya tohara kwa wanamume wote"

Katika siku ya tatu

"tatu" ni nambari za mpango kwa namba tatu. Inaweza kuwekwa bila nambari za mpango. "Baada ya siku mbili"

walipokuwa katika maumivu

"wakati wanamume wa mji walipokuwa bado na maumivu"

wakachukua kila mmoja upanga wake

"wakachukua panga zao"

kuushambulia mji

Hapa "mji" una maana ya watu. "waliwashambulia watu wa mji"

ulinzi wake, nao wakauwa wanamume wote

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. "ulinzi. Simoni na Lawi waliwaua wanamume wote wa mji ule"

kwa makali ya upanga

Hapa "makali" yana maana ya ubapa wa upanga. "kwa ubapa wa panga zao" au "kwa upanga wao"

Genesis 34:27

maiti

"maiti ya Hamori, Shekemu na wanamume wao"

pora mji

"waliiba kila kitu chenye thamani katika mji ule"

kwa sababu watu wale walikuwa wamemnajisi dada yao

Shekemu pekee alimnajisi Dina, lakini wana wa Yakobo walichukulia familia yote ya Shekemu na kila mtu katika mji kuhusika na tendo hili.

walikuwa wamemnajisi

Hii ina maana ya kwamba Shekemu alimvunjia heshima na kumuabisha sana Dina kwa kumlazimisha kulala naye.

Wakachukua makundi yao

"wana wa Yakobo wakachukua mifugo ya watu wale"

utajiri wao wote

"mali zao zote na fedha"

Watoto na wake zao wote, wakawachukua

"Waliwakamata watoto wao na wake zao wote"

Genesis 34:30

Mmeleta shida juu yangu

Kusababisha mtu kupitia shida inazungumziwa kana kwamba shida ilikuwa kitu kinacholetwa na kuwekwa juu ya mtu. "mmesababisha shida kubwa kwangu"

kunifanya ninuke kwa wenyeji wa nchi

Kusababisha watu katika maeneo yanayozunguka kumchukia Yakobo inazungumziwa kana kwamba wana wa Yakobo walimfanya anuke vibaya kihalisia. Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. "Mmenifanya nionekane kwa kinyaa kwa watu wanaoishi katika nchi"

Mimi nina watu wachache ... dhidi yangu na kunishambulia, kisha nitaangamizwa, mimi na nyumba yangu.

Hapa maneno "Mimi" na "yangu" yana maana ya nyumba yote ya Yakobo. Yakobo anasema "Mimi" au "yangu" kwa maana yeye ni kiongozi. "Nyumba yangu ni ndogo ... dhidi yetu na kutuvamia, kisha watatuangamiza sisi wote"

watajikusanya pamoja dhidi yangu na kunishambulia

"wataunda jeshi na kunishambulia" au "wataunda jeshi na kutushambulia"

kisha nitaangamizwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "wataniangamiza" au "watatuangamiza"

Je Shekemu alipaswa kumtendea dada yetu kama kahaba?

Simoni na Lawi wanatumia swali kusisitiza ya kwamba Shekemu alifanya kosa na alistahili kufa. "Shekemu hakupaswa kumtenda dada yetu kama kahaba!"

Genesis 35

Genesis 35:1

panda kwenda Betheli

Msemo "panda" unatumika kwa sababu Betheli ipo sehemu ya juu kuliko Shekemu.

Unijengee madhabahu pale

Mungu anaongea kuhusu yeye mwenyewe katika lugha ya utatu. "Jenga madhabahu pale kwangu, Mungu wako"

akawambia nyumba yake

"akwaambia familia yake"

Wekeni mbali miungu yote ya kigeni iliyo kati yenu

"Tupa mbali sanamu zenu" au "Zitokomeze miungu yenu ya uongo"

jitakaseni wenyewe, na kubadili mavazi yenu

Hii ilikuwa utamaduni wa kujitakasa kimaadili na kimwili kabla ya kwenda kumuabudu Mungu.

kubadili mavazi yenu

Kuvaa mavazi mapya ilikuwa ishara ya kwamba walijifanya safi kabla ya kumkaribia Mungu.

katika siku ya shida yangu

Maana za "siku" zaweza kuwa 1) siku ambayo Yakobo alimtoroka Esau au 2) "siku" ina maana ya kipindi ambacho Yakobo alikuwa na mawazo. "nilipokuwa katika kipindi kigumu" au "nilipokuwa katika shida"

Genesis 35:4

Hivyo wakampa

"kwa hiyo kila mmoja katika nyumba ya Yakobo akatoa" au "kwa hiyo kila mtu katika familia na watumishi walitoa"

iliyokuwa mikononi mwao

Hapa "mikononi mwao" ina maana ya kile walichomiliki. "kilichokuwa mali yao" au "walivyokua navyo"

heleni zilizokuwa katika masikio yao

"heleni zao". Maana zaweza kuwa 1) dhahabu katika heleni zingeweza kutumika sanamu zingine au 2) walichukua heleni hizi kutoka kwenye mji wa Shekemu baada ya kuishambulia na kuwaua watu wote. Heleni zingewakumbusha juu ya dhambi yao.

Mungu akaifanya miji yote iliyokuwa karibu nao kuhofu

Mungu kusababisha watu wa miji kumuogopa Yakobo na familia yake inazungumziwa kana kwamba "hofu" ilikuwa kitu kilichoanguka juu ya miji. Nomino inayojitegemea "hofu" inaweza kuwekwa kama "kuogopa". "Mungu aliwafanya watu waliozunguka miji kumuogopa Yakobo na wote aliokuwa nao"

miji yote

Hapa "miji" ina maana ya watu wanaoishi katika miji.

wana wa Yakobo

Inasemekana ya kwamba hakuna mtu aliyeshambulia familia ya Yakobo. Lakini wana wawili, Simoni na Lawi walishambulia ndugu wa Wakaanani wa Shekemu baada ya kumkamata na kulala na binti wa Yakobo. Yakobo aliogopa wangelipiza kisasi katika 34:30. "Familia ya Yakobo" au "Nyumba ya Yakobo"

Genesis 35:6

Luzu

Hili ni jina la mji.

El Betheli

"Jina la El Betheli lina maana ya "Mungu wa Betheli"

Mungu alikuwa amejifunua kwake

"pale Mungu alijifunua kwa Yakobo"

Debora

Hili ni jina la mwanamke.

mlezi wa Rebeka

Mlezi ni mwanamke ambaye humtunza mtoto wa mwanamke mwingine. Mlezi aliheshimika na alikuwa muhimu sana kwa familia.

Akazikwa chini kutoka Betheli

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Walimzika chini kutoka Betheli"

chini kutoka Betheli

Msemo "chini kutoka" unatumika kwa sababu walimzika katika eneo ambalo lilikuwa chini kwa mwinuko kuliko Betheli.

Aloni Bakuthi.

"Jina la Aloni Bakuthi lina maana ya "Mwaloni ambapo kuna maombolezo"

Genesis 35:9

Yakobo alipokuja kutoka Padani Aramu

Inaweza kuwekwa wazi ya kwamba walikuwa Betheli. "Baada ya Yakobo kuondoka Padani Aramu, na wakati alipokuwa Betheli"

kumbariki

Hapa "kubariki" ina maana ya kutamka baraka maalumu juu ya mtu na kusababisha mambo mazuri kutokea juu ya mtu huyo.

lakini jina lako halitakuwa Yakobo tena

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "lakini jina lako halitakuwa Yakobo tena"

Genesis 35:11

Mungu akamwambia

"Mungu akamwambia Yakobo"

Uwe mwenye kuzaa na kuongezeka

Mungu akamwambia Yakobo kuzaa watoto ili kwamba waweze kuwa wengi wao. Neno "kuongezeka" unaelezea jinsi anavyotakiwa "kuzaa".

Taifa na wingi wa mataifa watakujia, na wafalme watatoka miongoni mwa uzao wako

Hapa "taifa" na "mataifa" yana maana ya vizazi vya Yakobo ambao wataunda mataifa haya.

Mungu akapanda kutoka

Hapa "akapanda kutoka" inatumika kwa sababu Mungu anapoishi inafikiriwa kuwa juu au juu ya dunia. "Mungu akamuacha"

Genesis 35:14

nguzo

Hii ni nguzo ya ukumbusho ambayo ilikuwa jiwe au jabali kubwa iliyowekwa mwishoni pake.

Akamimina juu yake sadaka ya kinywaji na akamimina mafuta juu yake

Hii ni ishara ya kwamba anaweka wakfu nguzo kwa Mungu.

Betheli

"Jina la Betheli lina maana ya "nyumba ya Mungu".

Genesis 35:16

Efrathi

Hili ni jina lingine la mji wa Bethelehemu.

akashikwa na uchungu

"Alikuwa na wakati mgumu wakati alipokuwa akimzaa mtoto"

Alipokuwa katika utungu mzito zaidi

"Uchungu ulipokuwa katika hatua mbaya zaidi"

mkunga

mtu anayemsaidia mwanamke anapojifungua mtoto

Hata alipokaribia kufa, kwa pumzi yake ya mwisho

"pumzi yake ya mwisho" ni pumzi ya mwisho ya mtu kabla mtu hajafa. "Hata kabla hajafa, alipovuta pumzi yake ya mwisho"

Benoni

"Jina la Benoni lina maana ya "mtoto wa majonzi yangu""

Benyamini

Watafsiri wanaweza kuweka maandishi mafupi yasemayo "Jina la Benyamini lina maana ya "mtoto wa mkono wa kuume". Msemo wa "mkono wa kulia" unalenga sehemu yenye upendeleo maalumu.

na kuzikwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "na wakamzika"

katika njia

"pembeni mwa barabara"

ndiyo alama ya kaburi la Raheli hata leo

"inaweka alama juu ya kaburi la Raheli mpaka siku hii"

hata leo

"mpaka wakati huu wa leo." Hii ina maana hadi wakati ambapo mwandishi alikuwa akiandika haya.

Genesis 35:21

Israeli akaendelea

Inasemekana ya kwamba familia ya Israeli na watumishi wake wako pamoja naye. Maana kamili ya taarifa hii inaweza kuwekwa wazi.

Bilha

Hii ni jina la mtumishi wa Raheli wa kike.

Basi Yakobo alikuwa na wana kumi na mbili

Sentensi hii inaanza ibara mpya, ambayo inaendeleza mistari inayofuata.

wana kumi na mbili

"watoto 12"

Genesis 35:23

Bilha

Hili ni jina la mtumishi wa Raheli wa kike.

Genesis 35:26

Zilpa

Hili ni jina la mtumishi wa kike wa Lea.

waliozaliwa kwake huko Padani Aramu

Inasemekana ya kwamba hii haimjumlishi Benyamini aliyezaliwa katika nchi ya Kaanani karibu na Bethelehemu. Inataja Padani Aramu tu kwa maana hapo ndipo wengi wao walizaliwa. Maana kamili ya hii inaweza kuwekwa wazi. "ambao walizaliwa kwake Padani Aramu, isipokuwa Benyamini ambaye alizaliwa katika nchi ya Kaanani"

Yakobo akaja kwa Isaka

Hapa "akaja" inaweza kuweka kama "akaondoka"

Mamre

Hili lilikuwa jina lingine la mji wa Hebroni. Inawezekana iliitwa baada ya Mamre, rafiki yake Abrahamu aliyeishi pale. Hii ilikuwa jina la mwanamume aliyemiliki miti ya mwaloni.

Kiriathi Arba

Hili ni jina la mji.

Genesis 35:28

miaka mia moja na themanini

"miaka 180"

Isaka akapumua pumzi yake ya mwisho na akafa

"Isaka akapumua pumzi yake ya mwisho na akafa". Misemo ya "alivuta pumzi ya mwisho" na "akafa" ina maana ya kitu kimoja. "Abrahamu alikufa"

akapumua pumzi yake ya mwisho

Hii ni njia ya upole ya kusema mtu alikufa.

akakusanywa kwa wahenga wake

Hii ina maana ya kwamba baada ya Isaka kufa, roho yake ilikwenda sehemu ile ile ndugu zake waliokufa kabla yake. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "alijiunga na familia yake waliokuwa wamekufa"

mtu mzee amejaa siku

Misemo ya "mtu mzee" na "amejaa siku" zina maan moja. Zinasisitiza ya kwamba Isaka aliishi muda mrefu sana. "baada ya kuishi muda mrefu sana na kuzeeka sana"

Genesis 36

Genesis 36:1

Hivi ndivyo vizazi vya Esau (aliyeitwa pia Edomu)

"Hivi ndivyo vizazi vya Esau, ambaye pia anaitwa Edomu". Sentensi hii inatambulisha habari ya vizazi vya Esau katika Mwanzo 36:1-8. "Hii ni habari ya vizazi vya Esau, ambaye pia anaitwa Edomu"

Ada ... Oholibama

Haya ni majina ya wake wa Esau.

Eloni Mhiti

"Eloni kizazi cha Hethi" au "Eloni uzao wa Hethi". Hili ni jina la mwanamume.

Ana ... Zibeoni ... Nebayothi

Haya ni majina ya wanamume.

Mhivi

Hii ina maana ya kikundi kikubwa cha watu.

Basemathi

Hili ni jina la mke mmoja wa Esau.

Nebayothi

Hili ni jina la mtoto mmoja wa kiume wa Ishmaeli.

Genesis 36:4

Ada ... Basemathi ... Oholibama

Haya ni majina ya wake wa Esau.

Elifazi ... Reueli ... Yeushi ... Yalamu ... Kora

Haya ni majina ya wana wa Esau.

Genesis 36:6

aliyokuwa amekusanya katika nchi ya Kanaani

Hii ina maana ya vitu vyote vilivyokusanywa alipokuwa katika nchi ya Kaanani. "aliyokuwa amekusanya alipokuwa akiishi katika nchi ya Kanaani"

akaenda katika nchi

Hii ina maana ya kuhama katika sehemu nyingine na kuishi kule. "alikwenda kuishi katika nchi nyingine"

mali zao

"Mali za Esau na Yakobo"

isingeweza kuwafaa kwa mifugo yao. 8

Nchi haikuwa na ukubwa wa kutosha kuwatunza mifugo wote ambao Yakobo na Esau walimiliki. "haikuwa na ukubwa wa kutosha kuwatunza mifugo yao" au "haikuwa na ukubwa wa kutosha kwa mifugo ya Esau na Yakobo"

waliyokuwa wamekaa

Neno "wamekaa" lina maana ya kuelekea sehemu na kuishi pale. "pale walipohamia"

Genesis 36:9

Hivi ndivyo vizazi vya Esau

Sentensi hii inatambulisha habari ya vizazi vya Esau katika Mwanzo 36:9-43. "Hii ni habari ya vizazi vya Esau"

katika nchi ya mlima Seiri

Hii ina maana ya kwamba waliishi katika nchi ya mlima wa Seiri. Maana kamili ya hii inaweza kuwekwa wazi. "aliyeishi katika mlima wa nchi ya Seiri"

Elifazi ... Reueli

Haya ni majina ya wana wa Esau.

Ada ... Basemathi

Haya ni majina ya wake wa Esau.

Temani, Omari, Zefo, Gatamu, na Kenazi ... Amaleki

Haya ni majina ya wana wa Elifazi.

Timna

Hili ni jina la suria wa Elifazi.

Genesis 36:13

Reueli ... Yeushi, Yalamu, na Kora

Haya ni majina ya wana wa Esau.

Nahathi .... Zera ... Shama ... Miza

Haya ni majina ya wana wa Reueli.

Ana .... Zibeoni

Haya ni majina ya wanamume.

Basemathi ... Oholibama

Haya ni majina ya wake wa Esau.

Genesis 36:15

Elifazi

Hili ni jina la mwana wa Esau.

Temani, Omari, Zefo, Kenazi, Kora, Gatamu, na Amaleki

Haya ni majina ya wana wa Elifazi.

Ada

Hili ni jina la mmoja wa wake wz Esau.

Genesis 36:17

Reueli ... Yeushi, Yalamu, Kora

Haya ni majina ya wana wa Esau.

Nahathi, Zera, Shama, Miza

Haya ni majina ya wana wa Reueli.

katika nchi ya Edomu

Hii ina maana ya kwamba waliishi katika nchi ya Edomu. "walioishi katika nchi ya Edomu"

Basemathi ... Oholibama

Haya ni majina ya wake wa Esau.

Ana

Hili ni jina la mwanamume.

Genesis 36:20

Seiri

Neno la "Seiri" ni jina la mwanamume na nchi.

Mhori

Neno la "Mhori" lina maana la kundi la watu.

wakazi wa nchi hiyo

walioishi katika nchi ya Seiri, ambayo pia inaitwa Edomu.

Lotani, Shobali, Zibeoni, Ana, Dishoni, Ezeri, na Dishani ... Hori na Hemani

Haya ni majina ya wanamume.

Timna

Hili ni jina la mwanamke.

Genesis 36:23

Shobali ... Zibeoni

Haya ni majina ya wanamume.

Alvani, Manahathi, Ebali, Shefo, na Onamu ... Aia na Ana

Haya ni majina ya wanamume.

Genesis 36:25

Ana ... Dishoni ... Ezeri ... Dishoni

Haya ni majina ya wanamume.

Oholibama

Hili ni jina la mwanamke.

Hemdani, Eshbani, Ithrani, na Kerani ... ilhani, Zaavani, na Akani ... Uzi na Arani

Haya ni majina ya wanamume.

Genesis 36:29

Timna

Hili ni jina la kundi la watu.

Lotani, Shobali, Zibeoni, na Ana, Dishoni, Ezeri, Dishani

Haya ni majina ya wanamume.

katika nchi ya Seiri

Hii ina maana ya kwamba waliishi katika nchi ya Seiri. "kwa wale walioishi katika nchi ya Seiri"

Genesis 36:31

Bela ... Beori ... Yobabu ... Zera

Haya ni majina ya wanamume.

jina la mji wake

Hii ina maana ya kwamba huu ulikuwa mji ambapo aliishi. "jina la mji alipoishi"

Dinhaba ... Bozra

Haya ni majina ya mahali.

Genesis 36:34

Yobabu

Hili ni jina la mwanamume.

Hushamu ... Hadadi ... Bedadi ... Samla

Haya ni majina ya wanamume.

Hushamu aliyekuwa wa nchi ya Watemani

Hii ina maanisha Hushani aliishi katika nchi ya Watemani. "Hushami aliyeishi katika nchi ya Watemani"

Avithi ... Masreka

Haya ni majina ya mahali.

Watemani

"vizazi vya Temani"

Jina la mji wake

Hii ina maana ya kwamba huu ulikuwa mji ambao aliishi. "Jina la mji ambao aliishi"

Samla wa Masreka

"Samra wa Masreka"

Genesis 36:37

Samla

Hili ni jina la mwanamume.

kisha Shauli wa Rehobothi kando ya mto alitawala mahali pake

Shauli aliishi Rehobothi. Rehobothi ilikuwa karibu na Mto Frati. Taarifa hii inaweza kuwekwa wazi. "kisha Shauli akatawala katika nafasi yake. Alikuwa akitoka Rehobothi ambayo ipo karibu na Mto Frati"

Shauli ... Baali Hanani ... Akbori ... Hadari ... Matredi ... Me Zahabu.

Haya ni majina ya wanamume.

Rehobothi ... Pau

Haya ni majina ya mahali.

Jina la mji wake

Hii ina maana ya kwamba huu ulikuwa mji ambao aliishi. "Jina la mji ambao aliishi"

binti wa Matredi, mjukuu wa Me Zahabu.

Taarifa ambayo haionekani inaweza kuongezwa. "alikuwa binti wa Matredi, na mjukuu wa Me Zahabu"

Mehetabeli

Hili ni jina la mwanamke.

Genesis 36:40

majina ya wakuu wa koo

"viongozi wa koo zao"

kwa kufuata koo zao na maeneo yao, kwa majina yao

Koo na maeneo yalitajwa kwa majina ya viongozi wa koo zao. "jina la koo zao na maeneo walipoishi yalitajwa baada yao. Haya ndio majina yao"

Timna, Alva, Yethethi, Oholibama, Ela, Pinoni, Kenazi, Temani, Mbza, Magdieli, na Iramu

Haya ni majina ya makundi ya watu.

makazi

"makazi ya kuishi" au "sehemu waliokuwa wakiishi"

Huyu alikuwa Esau

orodha hii inasemekana "kuwa" Esau, ambayo ina maana ni orodha nzima ya vizazi vya Esau"

Genesis 37

Genesis 37:1

nchi aliyokaa babaye, katika nchi ya Kanaani

"katika nchi ya Kaanani ambapo baba yake aliishi"

Haya ndiyo matukio yaliyomhusu Yakobo

Sentensi hii inatambulisha habari ya watoto wa Yakobo katika Mwanzo 37:1-50:26. Hapa "Yakobo" ina maana ya familia yake nzima. "Hii ni habari ya familia ya Yakobo"

umri wa miaka kumi na saba

"umri wa miak 17"

Bilha

Hili ni jina la mtumishi wa kike wa Raheli.

Zilpa

Hili ni jina la mtumishi wa kike wa Lea.

wake

"suria". Wanawake hawa walikuwa watumishi wa Lea na Raheli waliopewa kwa Yakobo kumzalia watoto.

akaleta taarifa yao mbaya kuhusu wao

"taarifa mbaya kuhusu kaka zake"

Genesis 37:3

Basi

Neno hili linatumika hapa kuweka alama ya badiliko kutoka kwa simulizi kwenda kwa taarifa ya nyuma kuhusu Israeli na Yusufu.

akampenda

Hii ina maana ya upendo wa kindugu au upendo wa kirafiki au kifamilia. Huu ni upendo wa kawaida wa binadamu kati ya marafiki na ndugu.

wa uzee wake

Hii ina maana ya kwamba Yusufu alizaliwa wakati Israeli alikuwa mzee. "aliyezaliwa wakati Israeli alipokuwa mtu mzee"

Akamshonea

"Israeli alimshonea Yusufu"

vazi zuri

"joho zuri"

hawakuongea naye vema.

"hawakuweza kuongea kwa namna ya upole kwake"

Genesis 37:5

Yusufu akaota ndoto, na akawambia ndugu zake. Wakamchukia zaidi

Huu ni ufupi wa matukio ambayo yatatokea katika 37:6-11.

Wakamchukia zaidi

"Na kaka zake Yusufu walimchukia zaidi ya walivyomchukia hapo awali"

Tafadhari sikilizeni ndoto hii niliyoiota

"Tafadhali sikilizeni ndoto hii niliyoipata"

Genesis 37:7

Taarifa ya Jumla:

Yusufu anaeleza kaka zake kuhusu ndoto yake.

Tazama

Neno la "tazama" hapa linatuamsha kuvuta nadhari kwa taarifa ya kushangaza inayofuata.

tulikuwa

Neo "tulikuwa" ina maana ya Yusufu na inajumuisha kaka zake wote.

tukifunga miganda ya nafaka

Nafaka inapovunwa inafungwa katika makundi na kupangwa katika rundo hadi muda wa kuzitenga nafaka kutoka kwa majani makavu.

na tazama

Hapa neno "tazama" hapa linaonyesha ya kwamba Yusufu alishangazwa na kile alichokiona.

mganda wangu ukainuka na kusimama wima ... miganda yenu ikasogea na kuuinamia mganda wangu

Hapa miganda ya nafaka inasimama wima na kupiga magoti kana kwamba ilikuwa watu. Miganda hii inawakilisha Yusufu na kaka zake.

Je ni kweli utatutawala? Je utatutawala juu yetu?

Misemo hii miwili ina maana moja. Kaka zake Yusufu wanatumia swali kumkejeli Yusufu. Inaweza kuandikwa kama kauli. "Hutaweza kuwa mfalme wetu, na hatutainama chini kwako!"

utatutawala juu yetu

Neno la "yetu" lina maana ya kaka zake Yusufu lakini sio Yusufu.

kwa ajili ya ndoto zake na maneno yake

"kwa sababu ya ndoto yake na kile alichokisema"

Genesis 37:9

Akaota ndoto nyingine

"Yusufu akapata ndoto nyingine"

nyota kumi na moja

"nyota 11"

baba yake akamkemea. Akamwambia

"Israeli alimkaripia, akisema"

Je umeota ndoto ya namna gani hii? Je mama yako ... kukuinamia mpaka chini?

Israeli anatumia swali kumrekebisha Yusufu. Hii inaweza kuandikwa kama kauli. "Ndoto hii uliyoota sio ya kweli. Mama yako, kaka zako, na mimi hatutainama chini mbele yako!"

wivu

Hii ina maana kuwa na hasira kwa sababu mtu mwingine amefanikiwa au ana umaarufu zaidi.

akaliwema jambo hilo moyoni

Hii ina maana ya kwamba aliendelea kufikiria kuhusu maana ya ndoto ya Yusufu. "aliendelea kufikiria kuhusu maana ya ndoto ile"

Genesis 37:12

Je ndugu zako hawalichungi kundi huko Shekemu?

Israeli anatumia swali kuanza mazungumzo. Hii inaweza kuandikwa kama kauli. "Ndugu zako wanachunga kundi huko Shekemu".

Njoo

Hapa inasemekana ya kwamba Israeli anamuomba Yusufu kujiandaa kuondoka kuonana na ndugu zake. "Jiandae"

nipo tayari

Yupo tayari kuondoka. "Nipo tayari kuondoka"

Akamwambia

"Israeli akamwambia Yusufu"

uniletee neno

Israeli anamtaka Yusufu kurudi na kumuambia kuhusu kaka zake na hali ya mifugo. "njoo uniambie utakakikuta" au "niletee taarifa"

kutoka katika bonde

"kutoka bondeni"

Genesis 37:15

Mtu mmoja akamwona Yusufu. Tazama, Yusufu alikuwa akizunguka kondeni

"Mtu mmoja akamkuta Yusufu akizunguka kondeni"

Tazama

Hii inaweka alama mwanzo wa tukio jingine katika simulizi kuu. Inaweza kuhusisha watu tofauti kuliko matukio ya nyuma.

Unatafuta nini?

"Ni nini unatafuta"

Tafadhari, niambie, wapi

"Tafadhali niambie wapi"

wananalichunga kundi

"wakichunga kundi"

Dothani

Hili ni jina la mahali ambalo lipo kama kilomita 22 kutoka Shekemu.

Genesis 37:18

Wakamwona kutokea mbali

"Ndugu zake Yusufu wakamwona alipokuwa bado yupo mbali"

wakapanga njama ya kumwua

"wakafanya njama ya kumuua"

mwotaji anakaribia

"anakuja yule mwenye ndoto zile"

Njoni sasa

Msemo huu unaonyesha ya kwamba kaka zake walitekeleza mipango yao. "Kwa hiyo sasa"

Mnyama mkali

"mnyama wa hatari" au "mnyama mkali"

amemmeza

amemla kwa hamu

Nasi tutaona ndoto zake zitakuwaje

Ndugu zake walipanga kumuua, kwa hiyo ni kejeli kuzungumzia kuhusu ndoto zake kuwa kweli, maana angekuwa amekwisha kufa. "Kwa njia hiyo tutahakikisha ndoto zake haziji kuwa kweli"

Genesis 37:21

alilisikia

"alisikia walichokuwa wakisema"

kutoka katika mikono yao

Msemo "mikono yao" una maana ya mipango ya kaka zake ya kumuua. "kutoka kwao" au "kutoka kwa mipango yao"

Tusiuondoe uhai wake

Msemo wa "kuondoa uhai wake" ni tasifida kwa kumuua mtu. "Tusimuue Yusufu"

Msimwage damu

Ukanushaji unaweza kuwekwa juu ya kitenzi. Pia "kumwaga damu" ni tasifida ya kuua mtu. "Usimwage damu yoyote" au "Usimuue"

msiweke mikono yenu juu yake

Hii ina maana ya kumdhuru au kumjeruhi. "msimdhuru"

ili kwamba aweze kumwokoa

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. "Rubeni alisema hivi ili aweze kumuokoa Yusufu"

mikono mwao

Msemo wa "mikononi mwao" una maana ya mpango wa kaka zake kumuua. "kutoka kwao" au "kutoka kwa mipango yao"

kumrudisha

"na kumrudisha"

Genesis 37:23

Ikawa

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama juu ya tukio muhimu la simulizi.

walimvua vazi lake zuri

"walichana joho lake zuri kutoka kwake"

vazi lake zuri

"joho zuri"

Genesis 37:25

Wakakaa chini kula mkate

"Mkate" ni lugha nyingine kwa "chakula". "Walikaa chini kula chakula" au "Ndugu zake Yusufu walikaa chini kula"

Walipoinua macho yao na kuangalia, na, tazama, msafara

Hapa kuangalia juu inazungumziwa kana kwamba mtu aliinua macho yake juu kihalisia. Pia, neno "tazama" linatumika hapa kuvuta nadhari ya msomaji kwa kile walichokiona wanamume hawa. "Walitazama juu na ghafla wakaona msafara"

ulikuwa

"umebeba"

viungo

vikolezo

malhamu

kitu chenye mafuta chenye harufu tamu kinachotumiwa kwa ajili ya kuponya na kulinda ngozi. "dawa"

wakisafiri kuvichukua kuelekea Misri

"kuwaleta mpaka Misri". Hii inaweza kuwekwa wazi zaidi. "kuwaleta chini hadi Misiri kuviuza"

Ni faida gani kama tutamwua ndugu yetu na kufunika damu yake?

Hii inaweza kuandikwa kama kauli. "Hatupati faida yoyote kumuua ndugu yetu na kufunika damu yake"

kufunika damu yake

Huu ni msemo wenye maana ya kuficha kifo cha Yusufu. "kuficha mauaji yake"

Genesis 37:27

kwa Waishmaeli

"kwa wanamume hawa ambao ni vizazi vya Ishmaeli"

tusiweke mikono yetu juu yake

Hii ina maana ya kutomdhuru au kumjeruhi. "msimuumize"

ni ndugu yetu, nyama yetu

Neno la "nyama" ni lugha nyingine lenye maana ya ndugu. "ni ndugu wetu wa damu"

ndugu zake wakamsikiliza

"Kaka zake na Yuda walimsikiliza" au "Kaka zake Yuda walikubaliana naye"

Kimidiani ... Waishmaeli

Majina yote mawili yana maana ya kundi moja la wafanyabiashara ambao ndugu zake Yusufu walikutana nao.

kwa vipande ishirini vya fedha

"kwa bei ya vipande 20 vya fedha"

wakamchukua Yusufu mpaka Misri

"wakampeleka Yusufu Misri"

Genesis 37:29

Rubeni akarudi kwenye shimo, na, tazama, Yusufu hakuwemo shimoni

"Rubeni alirudi kwenye shimo, na akashangazwa kuona ya kwamba Yusufu hakuwepo mle" Neno "tazama" hapa linaonyesha ya kwamba Rubeni alishangazwa kukuta ya kwamba Yusufu aliondoka.

Akararua mavazi yake

Hili ni tendo la mawazo na uchungu mkubwa. Hii inaweza kuandikwa kwa uwazi zaidi. "Alikuwa na majonzi mpaka akararua nguo zake"

Kijana yuko wapi? Na mimi, je niende wapi?"

Rubeni anatumia maswali kuweka msisitizo kwa tatizo ambalo Yusufu hapatikani. Hivi vinaweza kuandikwa kama kauli. "Kijana ametoweka! Siwezi kurudi nyumbani sasa!"

Genesis 37:31

vazi la Yusufu

Hii ina maana ya joho zuri ambalo baba yake alimtengenezea.

damu

"damu ya mbuzi"

wakalipeleka

"walileta joho lile"

amemrarua

"amemla"

Yusufu ameraruliwa katika vipande.

Yakobo anadhani ya kwamba mnyama pori amerarua mwili wa Yusufu vipande vipande. "hakika imemchana Yusufu katika vipande vipande"

Genesis 37:34

Yakobo akararua mavazi yake

Hili ni tendo la mawazo na uchungu mkubwa. Hii inaweza kuandikwa kwa uwazi zaidi. "Yakobo alikuwa na majonzi mpaka akararua nguo zake"

kuvaa mavazi ya magunia katika viuno vyake

Hapa "viuno" ina maana ya sehemu ya katikati ya mwili au kiuno. "akavaa magunia"

wakainuka

Hapa ujio wa watoto kwa baba yao inazungumziwa kama "kuinuka juu". "wakaja kwake"

lakini alikataa kufarijiwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "lakini hakutaka wamfariji"

Hakika nitashuka kuzimu nikimwombolezea

Hii ina maana ataomboleza kutoka sasa hadi pale atakapokufa. "Kweli nitakapokufa na kwenda kuzimu bado nitakuwa naomboleza"

Wamidiani wakamwuza

"Wamidiani walimuuza Yusufu"

kepteni wa walinzi

"kiongozi wa wanajeshi waliokuwa wakimlinda mfalme"

Genesis 38

Genesis 38:1

Ikawa wakati ule Yuda

Hii inatambulisha sehemu mpya ya simulizi ambayo inamlenga Yuda.

Mwadulami fulani, jina lake Hira

Hira ni jina la mwanamume aliyeishi Adulami. Mwadulami ni utaifa wake.

jina lake Shua

Shua ni mwanamke wa Kaanani aliyeolewa na Yuda.

Genesis 38:3

Akawa mjamzito

"mke wa Yuda akawa mjamzito"

Akaitwa Eri

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Baba yake akamuita Eri"

Eri ... Onani ... Shela

Haya ni majina ya wana wa Yuda.

akamwita jina lake

"akamwita"

Kezibu

Hili ni jina la mahali.

Genesis 38:6

Eri

Hili ni jina la mmoja wa watoto wa Yuda.

alikuwa mwovu machoni pa Yahwe

Msemo "machoni pa" una maana ya yahwe kuona uovu wa Eri.. "alikuwa muovu na Yahwe akauona"

Yahwe akamwua

Yahwe akamuua kwa sababu alikuwa muovu. Hii inaweza kuwekwa wazi. "Kwa hiyo Yahwe akamuua"

Genesis 38:8

Onani

Hili ni jina la mmoja wa watoto wa Yuda.

Fanya wajibu wa shemeji kwake

shemeji kwake - Hii ina maana ya utamaduni ambao mwana mkubwa anapofariki kabla yeye na mkewe kupata mwana, ndugu anayefuata kiumri angemuoa na kulala na mjane. Mjane atakapozaa mwana wa kwanza, mtoto yule alijulikana kuwa mwana wa ndugu wa kwanza na angepokea urithi wa kaka wa kwaza.

lilikuwa ovu mbele za Yahwe

Msemo huu "machoni pa" una maana ya Yahwe kuona uovu wa Onani. "alikuwa muovu na Yahwe aliuona"

Yahwe akamwua pia

Yahwe akamuua kwa sababu alichofanya kilikuwa kiovu. Hii inaweza kuwekwa wazi. "Kwa hiyo Yahwe akamuua pia"

Genesis 38:11

mkwewe

mkwewe - "mke wa mwanawe mkubwa"

katika nyumba ya baba yako

Hii ina maana ya yeye kuishi katika nyumba ya baba yake. "na kuishi katika nyumba ya baba yako"

hadi Shela, mwanangu, atakapokuwa

Yuda anakusudia kwa Tamari kuja mumuoa Shela atakapokua mkubwa. "na pale ambapo Shela, mwanangu, atakapokua, ataweza kukuoa"

Shela

Hili ni jina la mmoja wa wana wa Yuda.

Kwani aliogopa, "Asije akafa pia, kama nduguze

Yuda aliogopa ya kwamba iwapo Shela atamuoa Tamari angekufa pia kama kaka zake walivyokufa. "Kwa maana alihofia, 'akimuoa na yeye angeweza kufa kama kaka zake walivyokufa"

Genesis 38:12

Shua

Hili ni jina la mwanamume.

Yuda akafarijika na

"Yuda alipokuwa haombolezi, ali"

wakatao kondoo wake manyoya huko Timna

"Timna, ambapo wanamume wake walikuwa wakinyoa manyoya ya kondoo"

Timna ... Enaimu

Haya ni majina ya mahali.

yeye na rafiki yake, Hira Mwadulami

"Rafiki yake Hirami, kutoka Adulami, alikwenda naye"

Hira Mwadulami

"Hira" ni jina la mwanamume, na "Adulami" ni jina la kijiji ambapo aliishi.

Tamari akaambiwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mtu akamwambia Tamari"

Tazama, mkweo

mkweo - "Sikiliza". Hapa neno "tazama" linatumika kushika nadhari ya Tamari.

mkweo

mkweo - "baba wa mume wako"

ya ujane

"ambayo wajane huvaa"

ushungi

kitambaa chembamba sana kinachotumika kufunika kichwa na uso wa mwanamke.

na akajifunika

Hii ina maana alijificha kwa nguo yake ili kwamba watu wasiweze kumtambua. Kitamaduni, sehemu za nguo za wanawake zilikuwa kubwa walizojizungushia nazo. "na akajifunika na kitambaa chake ili watu wasiweze kumtambua"

kando ya njia

"kando ya barabara" au "njiani"

hakupewa kuwa mke wake

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Yuda hakupatiwa kwa Shela kuwa mke"

Genesis 38:15

kwa maana alikuwa amefunika uso wake

Yuda hakufikiria ya kwamba alikuwa kahaba kwa sababu tu alifunika uso wake lakini pia kwa sababu alikuwa amekaa langoni. "kwa sababu alikuwa amefunika kichwa chake na kukaa mahali makahaba hukaa mara kwa mara"

Akamwendea kando ya njia

Tamari alikuwa amekaa kando ya njia. "Alikwenda mahali alipokuwa amekaa kando na njia"

Njoo

"Njoo kwangu" au "Njoo sasa"

Yuda alipomwona

"Yuda alipomwona Tamari"

mkwewe

mkwewe - "mke wa mwanawe"

Genesis 38:17

kutoka kwa kundi

"kutoka kwa kundi la mbuzi wangu"

Mhuri wako na mshipi ... fimbo

"Mhuri" ni sawa na sarafu yenye mchoro uliochongwa juu yake, unaotumika kuchapa nta iliyoyeyushwa. "Mshipi" uliwekwa katika mhuri ili kwamba mmiliki angeweza kuvaa shingoni mwake. Fimbo ilikuwa mti mrefu wa mbao uliosaidia kutembea juu ya ardhi ngumu.

Akawa na uja uzito wake

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "alimsababisha aweze kupata mimba"

Genesis 38:19

ushungi

kitambaa chembamba sana kinachotumika kufunika kichwa na uso wa mwanamke.

vazi la ujane wake

"ambayo wajane huvaa"

kutoka kundini

"kutoka katika kundi lake"

Mwadulami

"Adulami" ni jina la kijiji ambapo Hiramu aliishi.

aichukue rehani

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "chukua rehani"

kutoka katika mkono wa mwanamke

Hapa "mkono" unasisitiza ya kwamba vilikuwa katika umiliki wake. Mkono wa mwanamke una maana ya mwanamke. "kutoka kwa mwanamke"

Genesis 38:21

Mwadulami

"Adulami" ni jina la kijiji ambapo Hiramu aliishi.

watu wa sehemu

"baadhi ya wanamume ambao waliishi pale"

kahaba wa kidini

"kahaba aliyetumika katika hekalu"

Enaimu

Hili ni jina la mahali.

tusije tukaaibika

Watu wangekuja kugundua kilichotokea wangemkejeli Yuda na kumcheka. Hii inaweza kuwekwa wazi na kusemwa katika hali ya kutenda. "la sivyo watu watatucheka wakigundua kilichotokea"

Genesis 38:24

Ikawa

Msemo huu unatumika kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

Yuda akaambiwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "mtu akamwambia Yuda"

Tamari mkweo

mkweo - "Tamari, mke wa mwana wako mkubwa"

yeye ni mjamzito kwa tendo hilo

Hapa neno la "hilo" lina maana ya "ukahaba" alioufanya. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "limemfanya aweze kuwa na mimba" au "ana mimba"

Mleteni hapa

"Mleteni nje"

ili achomwe

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "tutamchoma mpaka kufa"

Alipoletwa nje

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Walipomleta nje"

mkwewe

mkwewe - "baba wa mume wake"

mhuri huu na mshipi na fimbo

"Mhuri" ni sawa na sarafu yenye mchoro uliochongwa juu yake, unaotumika kuchapa nta iliyoyeyushwa. "Mshipi" uliwekwa katika mhuri ili kwamba mmiliki angeweza kuvaa shingoni mwake. Fimbo ilikuwa mti mrefu wa mbao uliosaidia kutembea juu ya ardhi ngumu.

Shela

Haya ni majina ya wana wa Yuda.

Genesis 38:27

Muda ukafika

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

tazama

Neno "tazama" linatuamsha kwa mshtuko ya kwamba Tamari alikuwa amebeba mapacha, ambayo haikujulikana awali.

Muda wake wa kujifungua ukafika

Msemo huu "ukafika" unaweka alama kwa tukio muhimu katika simulizi.

mmoja akatoa mkono

"mmoja wa watoto akatoa mkono wake nje"

mkunga

Huyu ni mtu ambaye humsaidia mwanamke anayezaa mtoto.

kitambaa cha rangi ya zambarau

"kitambaa cha rangi nyekundu iliyoiva"

katika mkono wake

"kuzunguka kifundo cha mkono wake"

Genesis 38:29

Ikawa

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

tazama

Neno "tazama" hapa linatuamsha kuvuta nadhari kwa habari ya kushangaza inayofuata.

Umetokaje

Hii inaonyesha mshangao wa mkunga kuona mtoto wa pili akitoka kwanza. "Kwa hiyo hivi ndivyo unavyojitokeza kwanza!" au "Umejitokeza nje kwanza!"

akaitwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "akamuita"

Peresi

Hili ni jina la mtoto wa kiume. "Jina la Peresi lina maana ya "kuvunja nje".

Zera

Hili ni jina la mtoto wa kiume. "Jina la Zera lina maana ya "kitambaa cha rangi nyekundu".

Genesis 39

Genesis 39:1

Yusufu akaletwa chini Misri

Kusafiri kwenda Misri inasemekana mara kwa mara kama "chini" tofauti na kwenda "juu" katika nchi ya ahadi. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Muishmaeli alimchukua Yusufu mpaka Misri"

Yahwe alikuwa pamoja na Yusufu

Hii ina maana ya kwamba Yahwe alimsaidia Yusufu na alikuwa pamoja naye mara zote. "Yahwe alimuongoza Yusufu na kumsaidia"

Aliishi katika nyumba

Hapa mwandishi anazungumzia kufanya kazi ndani ya nyumba ya bwana wake kana kwamba alikuwa akiishi ndani ya nyumba ya bwana wake. Watumishi wanaoaminiwa pekee waliruhusiwa kufanya kazi ndani ya nyumba ya bwana wao. "alifanya kazi ndani ya nyumba".

Mmisri bwana wake

Yusufu sasa alikuwa mtumwa wa Potifa.

Genesis 39:3

Bwana wake akaona kwamba Yahwe alikuwa pamoja naye

Hii ina maana ya kwamba bwana wake aliona jinsi Yahwe alivyokuwa akimsaidia Yusufu. "Bwana wake aliona ya kwamba Yahwe alikuwa akimsaidia Yusufu"

kwamba Yahwe alifanikisha kila kitu alichokifanya

"Yahwe alisababisha kila kitu alichofanya Yusufu kufanikiwa"

Yusufu akapata kibali machoni pake

"Kupata kibali" ina maana ya kukubalika na mtu. Nomino ya "machoni pake" ina maana ya maoni ya mtu. Maana zaweza kuwa 1) "Potifa alifurahishwa na Yusufu" au 2) "Yahwe alifurahishwa na Yusufu"

Akamtumikia Potifa

Hii ina maana ya kwamba alikuwa mtumishi wa binafsi wa Potifa.

Potifa akamfanya msimamizi juu ya nyumba yake, na kila alichokimiliki

"Potifa alimweka Yusufu kusimamia nyumba yake na kila kitu kilichokuwa cha Potifa"

akakiweka chini ya uangalizi wake

Pale ambapo kitu "kinakuwa chini ya uangalizi wa mtu" ina maana ya kwamba mtu anawajibika na utunzanji na uhifadhi wake. "alimfanya Yusufu kutunza"

Genesis 39:5

Ikawa alipomfanya

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

alipomfanya msimamizi juu ya nyumba yake na juu ya kila kitu alichomiliki

"Potifa alimweka Yusufu kuwa msimamizi juu ya nyumba yake na juu ya kila kitu alichomiliki"

Baraka

Hapa "baraka" ina maana ya kusababisha mema na yenye manufaa kutokea kwa mtu au kitu kinachobarikiwa.

Baraka za Yahwe zilikuwa juu ya

Hapa mwandishi anazungumzia baraka ambayo Yahwe alitoa kana kwamba ilikuwa mfuniko wa kihalisia uliofunika kitu. "Yahwe alibariki"

kila kitu alichokuwa nacho Potifa nyumbani na shambani

Hii ina maana ya nyumba na nafaka na mifugo yake. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "Nyumba ya Potifa na nafaka na mifugo yake yote"

Potifa akaweka kila alichokuwa nacho chini ya uangalizi wa Yusufu

Kitu kinachokuwa "chini ya uangalizi wa mtu" ina maana ya kwamba mtu huyo anawajibika kutunza na kulinda. "Kwa hiyo Potifa alimweka Yusufu kuwa mwangalizi wa kila kitu ambacho alikuwa nacho"

Hakuwa na haja ya kufikiri juu ya lolote isipokuwa chakula alichokula tu.

Hakuhitaji kuwaza juu ya jambo lolote katika nyumba yake; alipaswa kufanya maamuzi juu ya kile alichotaka kula. Hii inaweza kuwekwa katika hali ya chanya. "Potifa alitakiwa kuwaza kuhusu kile alichotaka kula tu. Hakuhitaji kuwaza juu ya kitu kingine ndani ya nyumba yake"

Basi

Neno "basi" linaweka alama ya pumziko katika simulizi ambapo mwandishi anatoa taarifa ya nyuma kuhusu Yusufu.

mzuri na wa kuvutia

Maneno haya mawili yana maana moja. Yanalenga uzuri wa muenekano wa Yusufu. Yawezekana alikuwa mwenye sura nzuri na mwenye nguvu. "mwenye sura nzuri na nguvu"

Genesis 39:7

Ikawa baada ya hayo

"Na kwa hiyo". Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya tukio jipya katika simulizi.

Tazama

"Sikia". Yusufu anatumia neno hili kuvuta nadhari ya mke wa Potifa.

bwana wangu haangalii chochote nikifanyacho nyumbani

"bwana wangu hajishughulishi juu ya nyumba yake napokuwa msimamizi." Hii inaweza kuandikwa katika hali ya chanya. "bwana wangu ananiamini na nyumba yake"

ameweka kila kitu anachokimiliki chini ya uangalizi wangu

Kitu kinachokuwa "chini ya uangalizi wa mtu" ina maana ya kwamba mtu huyo anawajibika kutunza na kulinda. "Kwa hiyo Potifa alimweka Yusufu kuwa mwangalizi wa kila kitu ambacho alikuwa nacho"

Hakuna mtu aliye mkuu katika nyumba hii kuliko mimi

Hapa mwandishi anazungumzia juu ya mamlaka kana kwamba yalikuwa ukubwa. "Nina mamlaka katika nyumba hii kuliko mtu yeyote yule"

Hajanizuia chochote isipokuwa wewe

Hii inaweza kusemwa katika hali ya chanya. "Amenipatia kila kitu isipokuwa wewe"

Ni kwa namna gani basi naweza kufanya uovu mkuu namna hii na kumtenda dhambi Mungu?

Yusufu anatumia swali kuonyesha msisitizo. Hii inaweza kuandikwa kama kauli. "Hakika siwezi kufanya jambo hili ovu na kutedna dhambi dhidi ya Mungu"

Genesis 39:10

Alizungumza na Yusufu siku baada ya siku

Hii ina maana ya kwamba aliendelea kumuuliza kulala naye. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "Aliendelea kumuuliza Yusufu alale naye"

kuwa naye

"kuwa karibu naye"

Ikawa

"Na kwa hiyo". Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya sehemu mpya ya tukio katika simulizi.

Hakuna mtu yeyote wa nyumbani

"hakuna mwanamume yeyote aliyefanya katika nyumba"

akakimbia, na kutoka nje

"na akakimbia nje haraka" au "na kwa haraka akakimbia nje ya nyumba"

Genesis 39:13

Ikawa ... akawaita

"Kisha ... akawaita." Msemo "ikawa kwamba" unatumika hapa kuweka alama kwa tukio lifuatalo katika simulizi.

na kwamba amekimbia nje

"na kwa haraka alikimbia nje ya nyumba"

watu wa nyumbani mwake

"wanamume waliofanya kazi katika nyumba yake"

Tazama

"Sikiliza". Mke wa Potifa anatumia neno hili kuvuta nadhari ya watumishi wake.

Aliingia kulala nami

Hapa mke wa Potifa anamtuhumu Yusufu kwa kujaribu kumkamata na kulala naye.

Ikawa aliponisikia nikipiga kelele, akaniacha

"Ikawa aliponisikia nikipiga kelele, akaniacha". Msemo "ikawa kwamba" unatumika hapa kuweka alama kwa tukio lifuatalo la simulizi.

Genesis 39:16

bwana wake

"Bwana wa Yusufu." Hii ina maana ya Potifa.

Akamwambia maelelezo haya

"Alielezea namna hii"

uliyemleta kwetu

Neno hili "kwetu" ina maana ya Potifa, mke wake, na inamaanisha nyumba yake yote.

aliingia kunidhihaki

"alikuja ndani kunifanya mpumbavu". Hapa neno "dhihaki" ni tafisida ya "kumkamata na kulala naye". "alikuja nilipokuwepo na akajaribu kunilazimisha nilale naye"

Ikawa

"Kisha". Mke wa Potifa anatumiamsemo huu kuweka alama ya tukio linalofuata katika habari anayomwambia kuhusu Yusufu kujaribu kulala naye.

akakimbia nje

"alikimbia haraka nje ya nyumba"

Genesis 39:19

Ikawa

"Na kwa hiyo". Msemo huu unatumika kuweka alama ya tukio jipya katika simulizi.

bwana wake

"Bwana wake Yusufu". Hii ina maana ya Potifa. Taarifa hii inaweza kuwekwa wazi. "Bwana wake Yusufu, Potifa"

aliposikia maelezo aliyoambiwa na mkewe

"alimsikiliza mke wake akimuelezea kwake". Neno "wake" na "kwake" hapa yana maana ya Potifa.

alikasirika sana

"Potifa akawa na hasira sana"

mahali walipowekwa wafungwa wa mfalme

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "mahali ambapo mfalme huweka wafungwa wake"

Akawa pale

"Yusufu alikaa pale"

Genesis 39:21

Lakini Yahwe alikuwa pamoja na Yusufu

Hii ina maana ya namna Yahwe alivyomtunza Yusufu na kuwa mema kwake. "Lakini Yahwe alikuwa mwema kwa Yusufu" au "Lakini Yahwe alimtunza Yusufu"

Akampa kibali mbele ya mlinzi wa gereza

Hii ina maana Yahwe alisababisha mlinzi wa gereza kumkubali Yusufu na kumtendea wema. "Yahwe alisababisha mlinzi wa gereza kufurahishwa na Yusufu"

mlinzi wa gereza

"msimamizi wa gereza" au "mtu mwenye usamamizi na gereza"

akawaweka mikononi mwa Yusufu

Hapa "mkononi" unawakilisha nguvu ya Yusufu au uaminifu. "kumweka Yusufu juu ya"

Chochote walichokifanya, kilikuwa chini ya uangalizi wa Yusufu

"Yusufu alikuwa mwanaglizi wa kila kitu walichofanya pale"

kwa sababu Yahwe alikuwa pamoja naye

Hii ina maana ya jinsi Yahwe alivyomsaidia Yusufu na kumuongoza. "kwa sababu Yahwe alimuongoza Yusufu"

Yahwe akafanikisha kila alichokifanya.

"Yahwe alisababisha kila kitu ambacho Yusufu alifanya kufanikiwa"

Genesis 40

Genesis 40:1

Ikawa

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya tukio jipya la simulizi.

mnyweshaji

Huyu ni mtu ambaye huleta vinywaji kwa mfalme.

mwokaji wa mfalime

Huyu ni mtu ambaye alitengeneza chakula cha mfalme.

walimkosa bwana wao

"walimkwaza bwana wao"

maafsa wawili, mkuu wa wanyweshaji na mkuu wa waokaji

""mnyweshaji kiongozi na mwokaji kiongozi"

Akawaweka katika lindo katika nyumba ya kapteni wa walinzi

"Akawaweka katika gereza liliokuwa katika nyumba ambayo ilisimamiwa na kapteni wa walinzi"

Akawaweka

Mflame hakuwaweka gerezani lakini aliwaamuru wafungwe. "Akafanya wawekwe" au "Aliamuru walinzi wake kuwaweka"

katika gereza lile Yusufu alimofungwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Hili lilikuwa gereza lile lile ambalo Yusufu alikuwemo" au "Hili lilikuwa gereza lile lile ambalo Potifa alimweka Yusufu"

Genesis 40:4

Walikaa kifungoni kwa muda fulani

"Walikaa kifungoni kwa muda mrefu"

Genesis 40:6

Yusufu akaja kwao

"Yusufu akaja kwa mnyweshaji na mwokaji"

Tazama, walikuwa na uzuni

Neno "tazama" hapa linaonyesha ya kwamba Yusufu alishangazwa na kile alichokiona. "Alishangazwa kuona ya kuwa walikuwa na huzuni"

maafsa wa Farao waliokuwa pamoja naye

Hii ina maana ya mnyweshaji na mwokaji"

kifungoni katika nyumba ya bwana wake

"Gerezani katika nyumba ya bwana wake". "Bwana wake" ina maana ya bwana wa Yusufu, kapteni wa walinzi.

Je tafsiri haitoki kwa Mungu?

Yusufu anatumia swali kuonyesha msisitizo. Hii inaweza kuandikwa kama kauli. "tafsiri ni za Mungu!" au "Ni Mungu ambaye anaweza kusema maana ya ndoto!"

Niambieni, tafadhari

Yusufu anawaomba wamumbie ndoto zao. "Tafadhali niambieni ndoto"

Genesis 40:9

Mkuu wa wanyweshaji

Mtu muhimu zaidi ambaye huleta vinywaji kwa mfalme.

Katika ndoto yangu, tazama, kulikuwa na mzabibu mbele yangu

"Katika ndoto yangu, tazama, kulikuwa na mzabibu mbele yangu!" Mnyweshaji anatumia neno "tazama" hapa kuonyesha ya kwamba alishangazwa kwa kile alichokiona katika ndoto yake na kumuamsha Yusufu avute nadhari.

kuzaa vichala vya zabibu

"vichala vyake vikaiva kuwa zabibu"

kuzikamua

Hii ina maana ya kwamba alikamua juisi kutoka kwao. "akakamua juisi kutoka kwao"

Genesis 40:12

Tafsiri yake ni hii

"Hivi ndivyo ndoto inavyomaanisha"

Yale matawi matatu ni siku tatu

"Matawi matatu yanawakilisha siku tatu"

Ndani ya siku tatu

"Katika siku tatu zaidi"

atakiinua kichwa chako

Hapa Yusufu anaongea na Farao kumuachia mnyweshaji kutoka gerezani kana kwamba Farao alisababisha yeye kuinua kichwa chake. "atakuachia kutoka gerezani"

kukurudisha katika nafasi yako

"atakurudishia kazi yako"

kama ulivyokuwa

Maneno ambayo hayapo yanaweza kuongezwa. "kama ulivyofanya ulipokuwa"

Genesis 40:14

unionesha wema

"na tafadhali unioneshe wema kwangu"

Unitaje kwa Farao na kuniondoa hapa gerezani

Yusufu ana maana ya mnyweshaji kumwambia Farao juu yake ili kwamba Farao amfungulie kutoka gerezani. "Nisaidie kutoka katika gereza hili kwa kumwambia Farao juu yangu"

Maana hakika nilitekwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Maana hakika watu walinichukua" au "Maana hakika Waishmaeli walinichukua"

nchi ya Waebrania

"nchi ambayo Waebrania huishi"

hapa sijafanya chochote kinachonipasa niwekwe gerezani

"na pia nilipokuwa hapa Misri, sijafanya jambo lolote ambalo nastahili kuwekwa gerezani"

Genesis 40:16

Mkuu wa waokaji

Hii ina maana ya mtu kiongozi aliyetengeneza chakula cha mfalme.

Mimi pia niliota ndoto, na

"Mimi pia nilipata ndoto, na ndani ya ndoto yangu"

tazama, vikapu vitatu vya mikate vilikuwa juu ya kichwa changu

"kulikuwa na vikapu vitatu vya mikate juu ya kichwa changu!" Mwokaji anatumia neno "tazama" hapa kuonyesha ya kwamba alishangazwa kwa kile alichokiona ndani ya ndoto yake na kumuamsha Yusufu kuvuta nadhari.

bidhaa ya kuokwa kwa Farao

"alioka vyakula kwa ajili ya Farao"

Genesis 40:18

Tafsiri ni hii

"Hii ndio maana ya ndoto"

Vikapu vitatu ni siku tatu

"Vikapu vitatu vinawakilisha siku tatu"

atakiinua kichwa chako kutoka kwako

Yusufu pia alitumia msemo huu "atainua kichwa chako" alipoongea kwa mnyweshaji katika 40:12. Hapa ina maana tofauti. Maana zaweza kuwa 1) "atainua kichwa chako na kuweka kamba katika shingo yako" au 2) "atainua kichwa chako kukikata"

mwili

Hapa "mwili" una maana ya sehemu laini katika mwili wa mtu.

Genesis 40:20

Ikawa

"Hapo baadae, katika siku ya tatu". msemo "ikawa" unatumika hapa kuweka alama kwa tukio jipya katika simulizi.

Akafanya sherehe

"Akawa na sherehe"

mkuu wa wanyweshaji

Huyu alikuwa mtu kiongozi ambaye aliandaa na kuhudumia vinywaji kwa mfalme.

mkuu wa waokaji

Huyu alikuwa mtu kiongozi ambaye aliandaa chakula kwa ajili ya mfalme.

Akamrudisha mkuu wa wanyweshaji katika majukumu yake

"majukumu" wa mkuu wa wanyweshaji una maana ya kazi yake kama mkuu wa manyweshaji. "Alimrudishia mkuu wa wanyweshaji kazi yake"

Lakini akamtundika mkuu wa waokaji

Farao hakumnyonga mwokaji yeye binafsi, ila aliaamuru anyongwe. "Lakini aliamuru mkuu wa waokaji anyongwe" au "Lakini aliamuru walinzi wake kumnyonga mkuu wa waokaji"

kama Yusufu alivyokuwa amewatafsiria

Hii ina maana ya pale ambapo Yusufu alitafsiri ndoto zao. "kama vile Yusufu alivyosema kingetokea pale alipotafsiri ndoto za wanamume wale wawili"

Genesis 41

Genesis 41:1

Ikawa

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

mwishoni mwa miaka miwili mizima

Miaka miwili ilipita baada ya Yusufu kutafsiri kwa usahihi ndoto za mnyweshaji wa Farao na mwokaji, ambao walikuwa gerezani pamoja na Yusufu.

Tazama, alikuwa amesimama

Neno "tazama" hapa linaweka alama ya mwanzo wa tukio jipya katika simulizi kuu.

amesimama

"Farao alikuwa amesimama"

Tazama

"Ghafla". Neno la "tazama" hapa linaonyesha ya kwamba Farao alishangazwa kwa kile alichokiona.

wakupendeza na wanene

"wenye afya na wanene"

wakajilisha katika nyasi

"walikuwa wakila nyasi kando kando ya mto"

nyasi

nyasi ndefu, nyembamba ambazo huota katika maeneo ya unyevunyevu

Tazama, ng'ombe wengine saba

Neno "tazama" hapa linaonyesha ya kwamba Farao alishangazwa tena kwa kile alichokiona.

wasiopendeza na wamekondeana

"wagonjwa na wembamba"

ukingoni mwa mto

"kando kando ya mto" au "kando ya mto". Hii ni sehemu ya juu ya ardhi pembeni mwa mto.

Genesis 41:4

wasiopendeza na waliokonda

"dhaifu na nyembamba"

wanapendeza na walionenepa

"yenye afya na iliyolishwa vizuri"

akaamka

"aliamshwa"

mara ya pili

Neno "mara ya pili" ni mpangilio wa namba. "tena"

Tazama, masuke saba

Neno "tazama" hapa linaonyesha ya kwamba Farao alishangazwa kwa kile alichokiona.

masuke ya nafaka

Vichwa ni sehemu ya mmea wa mahindi ambao mbegu huota.

yalichipua katika mche mmoja

"yaliota katika shina moja" Shina ni sehemu nene au ndefu ya mmea.

katika mche mmoja, mema na mazuri

"katika mche mmoja na ilikuwa yenye afya na nzuri"

membamba na yaliyokaushwa na upepo wa mashariki

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ambayo ilikuwa nyembamba na kuchomwa kwa sababu ya upepo wa joto kutoka mashariki"

upepo wa mashariki

Upepo kutoka mashariki ulivuma kutoka jangwani. Joto la upepo wa mashariki mara kwa mara ulikuwa wenye uharibifu.

yakachipua

"yaliota" au "kukua"

Genesis 41:7

Masuke membamba

Maneno "ya mbegu" inaeleweka. "Vichwa vyembamba vya mbegu"

yakayameza

"wakala". Farao anaota ya kwamba mahindi ambayo hayana afya yanaweza kumeza mahindi yenye afya kama mtu anavyokula chakula.

masuke saba mema yote

"vichwa vyenye afya na vizuri"

akaamka

"aliamshwa"

tazama

Neno "tazama" hapa linaonyesha ya kwamba Farao alishangazwa na kile alichokiona.

ilikuwa ni ndoto

"alikuwa akiota"

Ikawa

Msemo huu unatumika kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

roho yake ikafadhaika

Hapa neno "roho" lina maana ya utu wake na hisia zake. "alifadhaishwa ndani ya utu wake" au "alisononeshwa"

Akatuma na kuwaita

Inaeleweka ya kwamba aliwatuma watumishi. "Alituma watumishi wake kuwaita" au "Aliwatuma watumishi wake na kuwaita"

waganga na wenye hekima wote wa Misri

Wafalme wa zamani na watawala walitumia wachawi na wenye hekima kama washauri.

Genesis 41:9

mkuu wa wanyweshaji

Mtu muhimu zaidi ambaye huleta vinywaji kwa mfalme.

Leo ninayafikiri makosa yangu

Neno "Leo" linatumika kuonyesha msisitizo. "makosa" yake ni kwamba alitakiwa kumwambia Farao kitu mapema zaidi lakini hakufanya hivyo. "Nimegundua ya kwamba nimesahau kukuambia jambo"

Farao aliwakasirikia

Mnyweshaji ana maana ya Farao katika mtu wa utatu. Hii ni njia ya kawaida ya mtu mwenye nguvu ya chini kuzungumza na mtu mwenye nguvu zaidi. "Wewe, Farao, ulikuwa na hasira"

watumishi wake

Hapa "wake" ina maana ya Farao. Hapa "watumishi" ina maana ya mnyweshaji na mkuu wa waokaji. "na sisi, watumishi wako"

kuniweka kifungoni katika nyumba ya kapteni wa walinzi, mkuu wa waokaji na mimi

"kuniweka mkuu wa waokaji na mimi gerezani ambapo kapteni wa walinzi alikuwa msimamizi" hapa "nyumba" ina maana ya gereza.

kapteni wa walinzi

Askari msimamizi wa walinzi wa kifalme.

mkuu wa waokaji

Mtu muhimu zaidi ambaye alitengeneza chakula kwa ajili ya mfalme.

Tuliota ndoto usiku huo mmoja, yeye na mimi

"Usiku mmoja wote wawili tulipata ndoto"

Tuliota

Hapa "Tuliota" ina maana ya mkuu wa mnyweshaji na mkuu wa waokaji.

Kila mmoja aliota kwa kadili ya tafsiri yake

"Ndoto zetu zilikuwa na maana tofauti"

Genesis 41:12

Taarifa ya Jumla:

Mkuu wa wanyweshaji anaendelea kuzungumza na Farao.

Pamoja nasi kulikuwa

"Gerezani kulikuwa na mkuu wa waokaji na mimi"

kapteni wa walinzi

Askari msimamizi wa walinzi wa kifalme.

Tulimwambia na akatutafsiria ndoto zetu

"Tulimwambia ndoto zetu na kutueleza maana zake kwetu"

Alitutafsiria kila mmoja wetu kulingana na ndoto yake

Hapa "yake" ina maana ya mnyweshaji na muokaji mmoja mmoja, sio kwa yule anayetafsiri ile ndoto. "Alifafanua kile kilichokuwa kinakuja kutokea kwetu wawili"

Ikawa

Msemo huu unatumika kuweka alama ya tukio muhimu la simulizi.

alivyotutafsiria, ndivyo ilivyokuwa

"alivyotafsiri kuhusu ndoto ndivyo kilichotokea hapo baadae"

Farao alinirudisha katika nafasi yangu

Hapa mnyweshaji anatumia jina la Farao katika kuongea naye kama njia ya kumheshimu yeye. "Uliniruhusu nirudi katika kazi yangu!"

yule mwingine

"mkuu wa waokaji"

akamtundika

Hapa "akamtundika" ina maana ya Farao. Na ina maana ya maaskari ambao Farao aliwaamuru kumnyonga mkuu wa waokaji. "uliwaamuru maaskari wako kumnyonga"

Genesis 41:14

Farao alipotuma na kumwita

Inaeleweka ya kwamba Farao aliwatuma watumishi. "Farao aliwatuma watumishi wake kumfuata Yusufu"

wakamtoa gerezani

"nje ya gereza" au "nje ya ile jela"

Akajinyoa mwenyewe

Ilikuwa utaratibu wa kawaida kunyoa ndevu na nywele za kichwani mnapoandaa kwenda mbele ya Farao.

akaingia kwa Farao

Hapa "akaingia" inaweza kuwekwa kama "kwenda". "alikwenda mbele ya Farao"

hakuna wa kuitafsiri

"hakuna awezaye kueleza maana yake"

unaweza kuitafsiri

"unaweza kuelezea maana yake"

Siyo katika mimi

"Mimi siye ambaye naweza kueleza maana yake"

Mungu atamjibu Farao kwa fadhila zake

"Mungu atamjibu Farao kwa fadhila"

Genesis 41:17

tazama, nilisimama

Farao anatumia neno "tazama" kumfanya Yusufu kuvuta nadhari kwa habari ya kushangaza.

ukingo wa mto Nile

Hii ni ardhi iliyo juuzaidi katika ukingo wa Mto Nile.

Tazama, ng'ombe saba

Farao anatumia neno "tazama" kumfanya Yusufu kuvuta nadhari kwa habari ya kushangaza.

wanene na wakuvutia

"waliolishwa vizuri na wenye afya"

wakajilisha katika nyasi

"walikuwa wakila nyasi kando ya mto"

Genesis 41:19

Tazama, ng'ombe wengine saba

Farao anatumia neno "tazama" kumfanya Yusufu kuvuta nadhari kwa habari ya kushangaza.

wabaya, na wembamba

"dhaifu, na wembamba"

wabaya kama hao

Nomino inayojitegemea ya "kutotamanika" inaweza kutafsiriwa kwa kivumishi. "ng'ombe wabaya sana" au "ng'ombe wasiofaa kabisa"

ng'ombe wanene

"ng'ombe waliolishwa vizuri"

haikujulikana kama walikuwa wamewala

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "hakuna aliyeweza kutambua ya kwamba ng'ombe wembamba waliwameza ng'ombe wanene"

Genesis 41:22

Taarifa ya Jumla:

Farao anaendelea kumwambia Yusufu ndoto zake.

Niliona katika ndoto yangu

Hii inaanza sehemu inayofuata ya ndoto ya Farao baadaya kuamka na kurudi kulala. "Kisha nikaota tena"

tazama, masuke saba

Farao anatumia neno "tazama" kumfanya Yusufu kuvuta nadhari kwa habari ya kushangaza.

masuke saba

Maneno "ya masuke" inaeleweka. "masuke saba"

yakatoka katika bua moja

"yakatoka katika bua moja". Shina ni sehemu ya mmea mnene na mrefu.

Tazama, masuke saba zaidi

Farao anatumia neno "tazama" kumfanya Yusufu kuvuta nadhari kwa habari ya kushangaza.

yaliyonyauka, membamba na yamekaushwa na upepo wa mashariki

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "yalinyauka, yamekaushwa, myembamba, na kukaushwa na jua kwa sababu ya upepo wa joto kutoka mashariki"

kunyauka

"kuoza" au "nyauka"

upepo wa mashariki

Upepo unaotoka kutoka mashariki ulivuma kutoka jangwani. Joto la upepo wa mashariki mara kwa mara ulikuwa uharibifu kwa mazao.

yakachipua

"yakaota" au "kustawi"

masuke membamba

Maneno "ya masuke" yanaeleweka. "masuke membamba"

yakayameza

"yakala". Farao anaota ya kwamba mahindi dhaifu yanaweza kumeza mahindi yenye afya kama mtu anavyokula chakula.

hakuna aliyeweza

"hapakuwa na mtu mmoja ambaye" au "hakuna kati yao ambaye"

Genesis 41:25

Ndoto za Farao zinafanana

Inadokezwa ya kwamba maana zinafanana. "Ndoto zote mbili zina maana moja"

Mungu amemwambia Farao kuhusu jambo analokwenda kulifanya

Yusufu anazungumza na Farao katika utatu. Kwa njia hii anaonyesha heshima. Inaweza kuwekwa katika upili wa mtu. "Mungu anakuonyesha kile atakachofanya hivi karibuni"

masuke saba mema

Maneno ya "masuke" yanaeleweka. "masuke saba mazuri"

Genesis 41:27

Taarifa ya Jumla

Yusufu anaendelea tafsiri yake kwa ndoto za Farao.

ng'ombe saba wembamba na wabaya

"ng'ombe wembamba na dhaifu"

masuke saba membamba yaliyokaushwa na upepo wa mashariki

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Masuke saba yaliyokaushwa na jua kwa sababu ya upepo wa joto kutoka mashariki"

Hilo ni jambo nililomwambia Farao ... nililomwambia Farao

Yusufu anazungumzia kwa Farao katika utatu. Hii ni njia ya kuonyesha heshima. Inaweza kuwekwa katika lugha ya upili. "Matukio haya yatatokea kama nilivyokuambia ... imefunuliwa kwako, Farao"

amemfunulia

"amefanya ijulikane"

Tazama

hii inatumika kuweka msisitizo kile ambacho Yusufu anachosema baadae. "Vuta nadhari kwa kile nachosema"

miaka saba yenye utele mwingi inakuja katika nchi yote ya Misri

Hii inazungumzia kuhusu miaka ya wingi kana kwamba muda ni kitu kinachosafiri na kufika mahali. "kutakuwa na miaka saba ambayo kutakuwa na chakula kingi katika nchi yote ya Misri"

Genesis 41:30

Taarifa ya Jumla

Yusufu anaendelea tafsiri ya ndoto za Farao.

miaka saba ya njaa itakuja baada yake

Hii inazungumzia kuhusu miaka saba ya njaa kana kwamba miaka ni kitu kinachosafiri na kufika mahali. "Kisha kutakuwa na miaka saba ambayo kutakuwa na chakula kichache"

wingi wote katika nchi ya Misri utasahaulika ... na njaa itaiaribu nchi. Wingi hautakumbukwa ... kwa sababu ya njaa itakayofuata

Yusufu anaonyesha wazo kwa njia mbili kusisitiza umuhimu wake.

wingi wote katika nchi ya Misri utasahaulika

Hapa "nchi" ina maana ya watu. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "watu wa Misri watasahau kuhusu miaka saba ambayo kulikuwa na chakula kingi"

itaiaribu nchi.

Hapa "nchi" ina maana ya udongo, watu, na nchi nzima.

kwa sababu ya njaa itakayofuata

Hii inazungumzia kuhusu njaa kana kwamba ilikuwa kitu kinachosafiri na kufuata nyuma ya kitu kingine. "kwa sababu ya muda wa njaa utakaotokea hapo baadae"

Kwamba ndoto ilijirudia kwa Farao sababu ni kwamba jambo hili limeanzishwa na Mungu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mungu alikupatia ndoto mbili kukuonyesha ya kwamba hakika atasababisha mambo haya kutokea"

Genesis 41:33

Maelezo ya Jumla:

Yusufu anaendelea kuongea na Farao.

Basi

Hii haimaanishi "katika kipindi hiki" lakini inatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.

Farao atafute

Yusufu anazungumza na Farao katika lugha ya utatu. Hii ni namna ya kuonyesha heshima. Inaweza kuwekwa katika lugha ya upili. "Wewe, Farao, unapaswa kutafuta"

kumweka juu ya nchi ya Misri

Msemo "kumweka juu" una maana ya kumpatia mtu mamlaka. "kumpatia mamlaka juu ya ufalme wa Misri" au "kumpa usimamizi juu ya ufalme wa Misri"

nchi ya Misri

Hapa "nchi" ina maana ya watu wote na kila kitu ndani ya Misri.

Na wachukue sehemu ya tano ya mazao ya Misri

Neno "tano" ni sehemu. "Na wagawanishe nafaka ya Misri katika sehemu tano za kufanana, kisha wachukue moja ya sehemu hizo"

katika miaka saba ya shibe

"katika miaka saba ambayo kutakuwa na wingi wa chakula"

Genesis 41:35

Maelezo ya Jumla

Yusufu anaendelea kumshauri Farao.

Na wakusanye

"Waruhusu wageni kukusanya"

cha hii miaka myema ijayo

Hii inazungumzia miaka kana kwamba ni kitu kinachosafiri na kufikia mahali. "katika miaka mizuri ambayo hivi karibuni itatokea"

kuitunza nafaka chini ya mamlaka ya Farao

Msemo "chini ya mamlaka ya Farao" ina maana ya Farao kuwapa mamlaka. "tumia mamlaka ya Farao kutunza nafaka"

Wakiifadhi

Hifadhi nafaka kwa muda wakati ambao kuna chakula kidogo. "Wasimamizi wanatakiwa kuwaacha walinzi pale kulinda nafaka"

Chakula kitakuwa akiba ya nchi

Hapa "nchi" ina maana ya watu. "Chakula hiki kitakuwa kwa ajili ya watu"

Kwa njia hii nchi haitaaribiwa na njaa

Hapa "nchi" ina maana ya watu. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Kwa njia hii watu hawatashinda njaa kipindi cha njaa"

Genesis 41:37

Ushauri huu ukawa mwema machoni pa Farao na machoni pa watumishi wake wote

Hapa "machoni" ina maana ya fikra na mawazo ya mtu. "Farao na watumishi wake walifikiri huu ulikuwa mpango mzuri"

watumishi wake

Hii ina maana ya watumishi wa Farao.

mtu kama huyu

"mtu kama vile Yusufu alivyomfafanua"

ambaye ndani yake kuna Roho wa Mungu

"ambaye Roho wa Mungu anaishi ndani mwake"

Genesis 41:39

hakuna mtu mwenye ufahamu

"hakuna mtu mwenye uwezo wa kufanya maamuzi"

Utakuwa juu ya nyumba yangu

Hapa "nyumba" ina maana ya kasri ya mfalme na watu ndani ya kasri. Msemo "utakuwa juu" una maana ya Yusufu kuwa na mamlaka juu ya. "Utakuwa na mamlaka juu ya kila mtu ndani ya kasri yangu"

watu wangu watatawaliwa kwa kadili ya neno lako

Hapa "neno" lina maana ya amri au kilichosemwa. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "utatawala juu ya watu wangu na wao watafanya kile unachoamuru"

kiti cha enzi peke yake

Hapa "enzi" ina maana ya utawala wa Farao kama mfalme. "Katika nafasi yangu pekee kama mfalme"

Tazama, nimekuweka

Neno "Tazama" linaweka msisitizo kwa kile Farao anachosema baadae. "Tazama, nimekuweka"

nimekuweka juu ya nchi yote ya Misri

Msemo "nimekuweka juu" una maana ya kutoa mamlaka. Hapa "nchi" ina maana ya watu. "Nimekuweka kuwa na mamlaka ya kila mtu ndani ya Misri"

Genesis 41:42

Farao akavua pete yake ya mhuri ... mkufu wa dhahabu shingoni mwake

Matendo haya yote yanaashiria ya kwamba Farao anampatia Yusufu mamlaka kufanya kila kitu ambacho Yusufu alipanga.

pete ya mhuri

Pete hii ilikuwa na mhuri wa Mfalme uliochongwa juu yake. Hii ilimpatia Yusufu mamlaka na fedha iliyohitajika kutekeleza mipango yake.

mavazi ya kitani safi

"Kitani" ni kitambaa kilaini, kigumu kinachotengenezwa na mmea wa kitani.

Akataka apandishwe katika kibandawazi cha pili alichokuwa nacho

Tendo hili linadhihirisha wazi kwa watu ya kwamba Yusufu ni wa pili tu kutoka kwa Farao.

Pigeni magoti

"Inama chini na mheshimu Yusufu". Kupiga goti na kuinama chini ilikuwa ishara ya heshima na taadhima.

Farao akamweka juu ya nchi yote

Msemo "kukuweka juu" una maana ya kumpatia mamlaka. Hapa "nchi" ina maana ya watu. "Nimekupa mamlaka juu ya kila mmoja ndani ya Misri"

Genesis 41:44

Mimi ni Farao, mbali na wewe

Farao anasisitiza mamlaka yake. "Kama Farao, ninaamuru hivi mbali na wewe"

mbali na wewe, hakuna mtu atakayeinua mkono wake au mguu wake katika nchi ya Misri

Hapa "nchi" na "mguu" zina maana ya matendo ya mtu. "hakuna mtu ndani ya Misri ataweza kufanya kitu chochote bila ruhusa yako" au "kila mtu ndani ya Misri lazima akuombe ruhusa kabla hajafanya jambo lolote"

hakuna mtu

Hapa "mtu" ina maana ya binadamu kwa ujumla, iwe wa kiume au wakike.

Zafenathi Panea

Jina la Zafenathi Panea kina maana ya "mfunuaji wa siri"

Akampa Asenathi, binti wa Potifera kuhani wa On, kuwa mke wake

Makuhani wa Misri walikuwa tabaka la juu kabisa na upendeleo. Ndoa hii inaashiria nafasi ya Yusufu ya heshima na upendeleo.

Akampa Asenathi

"Asenathi" ni jina la mwanamke ambaye Farao alimpatia Yusufu kuwa mke wake.

binti wa Potifera

"Potifera" ni baba wa Asenathi.

kuhani wa Oni

Oni ni mji, ambao pia unajulikana kama Heliopolisi, ambao ulikuwa "Mji wa Jua" na makao ya kumuabudu mungu wa jua Ra.

Yusufu akaenda juu ya nchi yote ya Misri

Yusufu alisafiri katika nchi kusimamia maandalizi ya ujio wa ukame.

Genesis 41:46

umri wa miaka thelathini

"umri wa miaka 30"

aliposimama mbele ya Farao

Hapa "aliposimama" ina maana ya Yusufu kuanza kumtumikia Farao. "alipoanza kumtumikia Farao"

kwenda katika nchi yote ya Misri

Yusufu anakagua nchi anapoandaa kutekeleza mipango yake.

Katika miaka saba ya shibe

"Katika miaka mizuri saba"

nchi ilipozaa kwa wingi

"nchi ilizaa mavuno makubwa"

Genesis 41:48

Akakusanya ... kukiweka

Hapa "Akakusanya" ina maana ya watumishi wa Yusufu. "Yusufu aliwaamuru watumishi wake kukusanaya ... Wakaweka"

Yusufu akahifadhi nafaka kama mchanga wa bahari

Hii inalinganisha nafaka na mchanga wa bahari kuweka msisitizo wa idadi yake kubwa. "Nafaka ambayo Yusufu alihifadhi ilikuwa nyingi kama mchanga wa baharini.

Yusufu akahifadhi ... akaacha

Hapa "Yusufu" na "akahifadhi" ina maana ya watumishi wa Yusufu. "Yusufu aliwafanya watumishi wake wahifadhi ... wakaacha"

Genesis 41:50

Kabla miaka ya njaa kuingia

Hii inazungumzia kuhusu miaka saba kana kwamba ni kitu kinachosafiri na kuja kutulia mahali. "kabla ya miaka saba ya njaa kuanza"

Asenathi

"Asenathi" ni jina la mwanamke ambaye Faro alimpatia Yusufu kama mke wake.

binti wa Potifera

"Potifera" ni baba wa Asenathi.

kuhani wa Oni

Oni ni mji, ambao pia unajulikana kama Heliopolisi, ambao ulikuwa "Mji wa Jua" na makao ya kumuabudu mungu wa jua Ra.

Manase

"Jina la 'Manase' lina maana ya "kusababisha kusahau""

nyumba ya baba yake

Hii ina maana ya baba wa Yusufu Yakobo na familia yake.

Efraimu

"Jina la 'Efraimu' lina maana ya 'kuwa na uzao' au 'kupata watoto'"

amenipa uzao

Hapa "uzao" ina maana ya kufanikiwa au kupata watoto.

katika nchi ya mateso yangu

Nomino inayojitegemea "mateso" inaweza kuwekwa kama "nimeteseka". "katika nchi hii ambayo nimeteseka".

Genesis 41:53

katika nchi yote

Katika mataifa yanayozunguka mbele zaidi ya Misri, kujumuisha na nchi ya Kanaani.

lakini katika nchi yote ya Misri kulikuwa na chakula

Inasemekana ya kwamba kulikuwa na chakula kwa sababu Yusufu aliwaamuru watu wake kuhifadhi chakula katika kipindi cha miaka saba mizuri.

Genesis 41:55

Nchi yote ya Misri ilipokuwa na njaa

Hapa "nchi" ina maana ya watu. "Ambapo Wamisri waliposhikwa na njaa"

Njaa ilikuwa juu ya uso wote wa nchi

Neno "uso" lina maana ya sehemu ya juu ya ardhi. "Njaa ilisambaa katika nchi yote"

Yusufu akafungua ghala zote na kuuza chakula kwa Wamisri

Hapa "Yusufu" ina maana ya watumishi wa Yusufu. "Yusufu aliwafanya watumishi wake kufungulia maghala yote na kuuza nafaka kwa Wamisri"

Dunia yote ilikuwa inakuja Misri

Hapa "dunia" ina maana ya watu kutoka maeneo yote. "Watu walikuwa wakija Misri kutoka maeneo yaliyozunguka"

katika dunia yote

"katika nchi yote". Inawezekana ya kwamba wafanyabiashara tofauti na mataifa ambayo yalikuwa sehemu ya njia za biashara na Misri yalioguswa na ukame walikuja Misri kwa ajili ya nafaka.

Genesis 42

Genesis 42:1

Basi Yakobo akafahamu

Neno "basi" inaweka alama ya sehemu mpya ya simulizi.

Kwa nini mnatazamana?

Yakobo anatumia swali kukaripia watoto wake kwa kutofanya kitu chochote kuhusu nafaka. "Msikae hapo tu!"

Shukeni huko ... chini

Ilikuwa kawaida kuzungumza kuhusu kwenda kutoka Kaanani mpaka Misri kama kwenda "chini"

kutoka Misri

Hapa "Misri" ina maana ya watu kuuza nafaka. "kutoka kwa wale wauzao nafaka ndani ya Misri"

Benjamini, ndugu wa Yusufu, Yakobo hakumtuma

Benyamini na Yusufu walikuwa na baba mmoja na mama. Yakobo hakutaka kuthubutu kumtuma mwanawe wa mwisho wa Raheli.

Genesis 42:5

Wana wa Israeli wakaja kununua miongoni mwao waliokuja

Neno "wakaja" inaweza kutafsiriwa kama "kwenda". Pia, maneno "nafaka" na "Misri" inaeleweka. "Wana wa Israeli walikwenda kununua nafaka pamoja na watu wengine waliokwenda Misri"

Basi Yusufu

"Basi" inaweka alama ya badiliko kutoka kwa simulizi kwenda kwa maelezo ya nyuma kuhusu Yusufu.

juu ya nchi

Hapa "nchi" ina maana ya Misri. "juu ya Misri"

watu wote wa nchi

Hapa "nchi" inajumlisha Misri na nchi zingine zinayoizunguka. "watu wote wa mataifa yote waliokuja kununua nafaka"

Ndugu zake Yusufu wakaja

Hapa "wakaja" inaweza kutafsiriwa kama "walikwenda"

kumwinamia na nyuso zao hata chini

Hii ni njia ya kuonyesha heshima.

Genesis 42:7

Yusufu akawaona ndugu zake na kuwatambua

"Yusufu alipowaona ndugu zake, aliwatambua"

alijibadili kwao

"alijifanya kana kwamba hakuwa kaka yao" au "hakuwafahamisha ya kwamba alikuwa kaka yao"

Mmetoka wapi?

Hili halikuwa swali la balagha ingawa Yusufu alijua jibu. Ilikuwa sehemu ya maamuzi yake kuficha utambulisho wake kwa ndugu zake.

Genesis 42:9

Ninyi ni wapelelezi

Wapelelezi ni watu ambao kwa siri hujaribu kupata taarifa kuhusu nchi ili kuisaidia nchi nyingine.

Mmekuja kuona sehemu za nchi

Maana kamili inaweza kuwekwa wazi. "Mmekuja kujua ni wapi hatulindi nchi yetu ili kwamba muweze kutushambulia"

bwana wangu

Hii ni njia ya kuonyesha heshima kwa mtu.

Watumishi wako wamekuja

Ndugu hawa wanajitambulisha kama "watumishi". Hii ni njia maalumu ya kuongea na mtu mwenye mamlaka makubwa zaidi. "Sisi, watumishi wako, tumekuja" au "Tumekuja"

Genesis 42:12

Akawambia

"Yusufu akawaambia ndugu zake"

Hapana, mmekuja kuangalia sehemu za nchi

Maana kamili inaweza kuwekwa wazi. "Hapana, mmekuja kujua ni wapi hatujalinda nchi yetu ili kwamba muweze kutuvamia"

ndugu kumi na wawili

"ndugu 12"

Tazama, mdogo

"Tusikilize, mdogo". Neno "Tazama" linatumika kusisitiza kile walichosema baadae.

mdogo yupo na baba yetu leo hii

"kwa sasa ndugu yetu mdogo yupo na baba yetu"

Genesis 42:14

Ndivyo nilivyowambia; ninyi ni wapelelezi

"kama nilivyotangulia kusema, nyinyi ni wapelelezi"

Mtajaribiwa kwa njia hii

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Hivi ndivyo nitakavyowajaribu"

aishivyo Farao

Msemo huu unaashiria kiapo maalumu.

Mtumeni mmoja wenu amlete mdogo wenu

"Chagueni mmoja wenu kumfuata mdogo wenu"

Mtabaki gerezani

"Mliosalia mtabaki gerezani"

hata maneno yenu yatakapothibitishwa, kama kuna ukweli ndani yenu.

Hapa "maneno" ina maana ya kile alichosema. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ili kwamba niweze kujua kama mnaniambia ukweli"

kifungoni

"gerezani"

Genesis 42:18

Katika siku ya tatu

Neno "tatu" ni mpangilio wa namba."baada ya siku ya pili"

Fanyeni hivi nanyi mtaishi

Taarifa inayotambulika inaweza kuwekwa wazi. "Kama utafanya kile nilichosema, nitakuruhusu uishi"

ninamcha Mungu

Hii ina maana ya kumheshimu Mungu kwa dhati na kuonyesha heshima hiyo kwa kumtii yeye.

mmoja wenu atazuiliwa hapa gerezani

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "muache mmoja wa ndugu zako hapa gerezani"

lakini ninyi nendeni

Hapa "ninyi" ni wingi na ina maana ya ndugu wote ambao hawatakaa gerezani. "lakini ninyi mliosalia"

chukueni nafaka kwa ajili ya nyumba zenu

Hapa "nyumba" ina maana ya familia. "beba nafaka hadi nyumbani kusaidia familia zenu wakati wa njaa hii"

ili kwamba maneno yenu yathibitishwe

Hapa "maneno" yana maana ya kile kilichosemwa. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ili niweze kujua kile mnachosema ni kweli"

nanyi hamtakufa

Hii inaashiria ya kwamba Yusufu angewafanya maaskari wake kuwaua ndugu iwapo angetambua ya kwamba walikuwa wapelelezi.

Genesis 42:21

kwani tuliona tabu ya nafsi yake

Neno "nafsi" ina maana ya Yusufu. "kwa sababu tuliona jinsi gani Yusufu alivyotaabika" au "kwa sababu tuliona ya kwamba Yusufu aliteseka"

Kwa hiyo taabu hii imeturudia

Nomino inayojitegemea "taabu" inaweza kuwekwa kama kitenzi "kuteseka" "Ndio maana tunateseka hivi sasa"

Je sikuwambia, 'Msitende dhambi juu ya kijana,' lakini hamkusikia?

Rubeni anatumia swali kuwakaripia ndugu zake. "Niliwaambia kutomuumiza kijana, lakini hamkunisikiliza!"

Je sikuwambia, 'Msitende dhambi juu ya kijana'

Hii inaweza kuwa nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Je sikuwaambia msimtendee dhambi kijana" au "Niliwaambia msimdhuru kijana"

Basi, tazama

Hapa "basi" haimaanishi "katika muda huu" lakini yote maneno "Sasa" na "tazama" yanatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.

damu yake inatakiwa juu yetu

Hapa "damu" ina maana ya kifo cha Yusufu. Ndugu zake walidhani Yusufu alikufa. Msemo "inatakiwa juu yetu" una maana wanatakiwa kuadhibiwa kwa kile walichokifanya. "tunapata kile tunachostahili kwa kifo chake" au"tunateseka kwa kumuua yeye"

Genesis 42:23

hawakuja ... mkalimani kati yao

Hii inabadilisha kutoka kwenye simulizi kuu kwenda kwenye taarifa ya nyuma ambayo inaelezea kwa nini ndugu walidhani Yusufu hakuweza kuwaelewa.

mkalimani

"Mkalimani" ni mtu ambaye hutafsiri kile mtu anazungumza katika lugha nyingine. Yusufu aliweka mkalimani kati yake na ndugu zake kufanya ionekane kana kwamba hakuzungumza lugha yake.

Akatoka kwao na kulia

Inasemekana ya kwamba Yusufu alilia kwa sababu alipatwa na hisia baada kusikia walichosema ndugu zake.

kuongea nao

Yusufu aliendelea kuzingumza katika lugha nyingine na kutumia mkalimani kuzungumza na ndugu zake.

kumfunga mbele ya macho yao

Hapa "macho" ina maana ya machoni mwao. "alimfunga machoni mwao" au "alimfunga huku wakitazama"

na kuwapa mahitaji

"kuwapatia mahitaji waliyohitaji"

Wakatendewa hivyo

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. Watumishi walifanya kwao kila kitu ambachoYusufu aliwaamuru"

Genesis 42:26

Mmoja wao alipofungua gunia lake ili kumlisha punda wao katika sehemu waliyokuwa, akaona pesa yake. Tazama, ilikuwa mdomoni mwa gunia lake

"Waliposimama mahali usiku huo, mmoja wa ndugu alifungua gunia lake kupata chakula kwa ajili ya punda wake. Ndani ya gunia akakuta fedha!"

Tazama

Neno "tazama" hapa linatuamsha kuvuta nadhari kwa taarifa inayoshangaza inayofuata.

Pesa yangu imerudishwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mtu amerudisha fedha yangu"

Tazama

"Tazama ndani ya gunia langu!"

Mioyo yao ikazimia

Kuwa na hofu inazungumziwa kana kwamba mioyo yao ilikuwa ikizama. Hapa "mioyo" ina maana ya ujasiri. "Wakawa na hofu sana"

Genesis 42:29

bwana wa nchi

"bwana wa Misri"

aliongea nasi kwa ukali

"aliongea kwa jazba"

kuwa wapelelezi

Wapelelezi ni watu ambao kwa siri hujaribu kupata taarifa kuhusu nchi ili kuisaidia nchi nyingine.

Tukamwambia, 'Tu watu wa kweli sisi. Sisi siyo wapelelezi. Tupo ndugu kumi na wawili, wana wa baba yetu. Mmoja hayupo hai tena ... nchi ya Kanaani

Hii ina nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Tulimwambia ya kwamba sisi ni watu waaminifu na sio wapelelezi. Tulisema kwamba tu ndugu kumi na wawili, wana wa baba yetu, na kwamba ndugu yetu hayupo hai tena ... nchi ya Kaanani"

Mmoja hayupo hai tena

Neno "ndugu" linaeleweka. "Ndugu mmoja hayupo hai tena"

mdogo yupo na baba yetu

Neno "ndugu" linaeleweka. "ndugu yetu mdogo yupo na baba yetu kwa sasa"

Genesis 42:33

bwana wa nchi

"bwana wa Misri"

chukueni chakula kwa ajili ya njaa katika nyumba zenu

Hapa "nyumba" ina maana ya "familia". "chukua nafaka isaidie familia yenu wakati wa njaa"

mwondoke

"nendeni nyumbani" au "ondokeni"

na mtafanya biashara katika nchi

"na nitawaruhusu mnunue na kuuza katika nchi hii"

Genesis 42:35

Ikawa

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama kwa tukio muhimu katika simulizi.

tazama

"kwa mshangao wao". Neno "tazama" hapa inaonyesha ya kwamba ndugu walishangazwa kwa kile walichokiona.

Mmeniharibia watoto wangu

"umeninyima watoto wangu" au "umesababisha kupoteza watoto wangu wawili"

Mambo haya yote ni kunyume changu

"mambo haya yote yaliniumiza"

Genesis 42:37

Mweke mikononi mwangu

Hili ni ombi la Rubeni kumchukua Benyamini pamoja naye na kumtunza katika safari hiyo. "Niweke kama msimamizi juu yake" au "Niache nimtunze"

Mwanangu hatashuka pamoja nanyi

Ilikuwa kawaida kutumia msemo "kushuka" walipokuwa wakizungumzia safari ya Kaanani kuelekea Misri. "Mwanangu, Benyamini, hatakwenda nawe hadi Misri"

pamoja nanyi

Hapa "nanyi" ni wingi na ina maana ya wana wa yakobo wakubwa.

Kwani ndugu yake amekufa na yeye peke yake amebaki

Maana kamili inaweza kuwekwa wazi. "Kwa maana mke wangu, Raheli, alikuwa na watoto wawili pekee. Yusufu amekufa na Benyamini amebaki mwenyewe tu"

katika njia mnayoiendea

"utakapokuwa ukisafiri kwenda Misri na kurudi" au "utakapokuwa mbali". Hapa "njia" ina maana ya kusafiri.

ndipo mtakapozishusha mvi zangu kaburini kwa huzuni

"mtakapozishusha ... kuzimu" ni njia ya kusema watamsababisha afariki na kushuka kuzimu. Anatumia neno "chini" kwa sababu iliaminika kuzimi ni sehemu chini ya ardhi. "basi mtanisababisha, mtu mzee, kufariki na huzuni"

mvi zangu

Hii ina maana ya Yakobo na inasisitiza umri wake mkubwa. "mimi, mtu mzee"

Genesis 43

Genesis 43:1

Njaa ilikuwa kali katika nchi

Neno "Kaanani" linaeleweka. Taarifa hii inaweza kuwekwa wazi. "Njaa ilikuwa kali katika nchi ya Kaanani"

Ikawa

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

walipokuwa wametumia chakula

"Yakobo na familia yake walipokuwa wamekula"

walichokitoa

"wana wakubwa wa Yakobo walileta"

mtununulie

Hapa "mtununulie" ina maana ya Yakobo, wanawe, na familia yake iliyobaki.

Genesis 43:3

Yuda akamwambia

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "alituonya ya kwamba hatutauona uso wake hadi tumlete ndugu yetu mdogo pamoja nasi"

Yule mtu

Hii ina maana ya Yusufu, lakini ndugu hawakujua alikuwa Yusufu. Walimtaja kama "mtu" au "yule mtu, bwana wa nchi" kama katika 42:29.

alituonya, "Hamtauona uso wangu ndugu yenu asipokuwa nanyi"

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "alituonya ya kwamba hatutauona uso wake hadi tumlete ndugu yetu mdogo pamoja nasi"

alituonya kwa ukali

"alikuwa na hali ya ukali alipotuonya, akisema"

Hamtauona uso wangu

Yuda anatumia msemo huu mara mbili katika 43:3-5 kuweka msisitizo kwa baba yake ya kwamba hawawezi kurudi Misri bila Benyamni. Msemo "uso wangu" una maana ya yule mtu, ambaye ni Yusufu. "Hamtaniona"

ndugu yenu awe nanyi

Yuda ana maana ya Benyamini, mtoto wa Raheli wa mwisho kabla yeye hajafa.

hatutashuka

Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "kushuka" kuzungumzia safari ya Kaanani kwenda Misri.

Genesis 43:6

Kwa nini mlinitendea mimi vibaya hivyo

"Kwa nini mlinisababishia matatizo makubwa hivi"

Yule mtu alituuliza habari zetu

"Yule mtu aliuliza maswali mengi"

juu yetu

Hapa "yetu" inajitegemea na ina maana ya ndugu waliokwenda Misri na kuzungumza na"yule mtu".

Akasema, 'Je baba yenu bado yuko hai? Je mnaye ndugu mwingine?

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Alituuliza kwa kuzunguka kama baba yetu alikuwa bado yu hai na kama tuna ndugu mwingine".

Tukamjibu kulingana na maswali haya

"Tulimjibu maswali aliyotuuliza"

Tungejuaje kwamba angetwambia, 'Mleteni ndugu yenu

Wana hawa wanatumia swali kuweka msisitizo ya kwamba hawakujua ni kitu gani yule mtu angewaambia kufanya. Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Hatukujua ya kwamba angetuambia ... chini!"

angetwambia, 'Mleteni ndugu yenu?"

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "angetuambia kumfuata ndugu yetu huku chini Misri"

Mleteni ndugu yenu chini

Ilikuwa kawaida kutumia neno la "chini" katika kuzungumzia safari ya kutoka Kanaani kwenda Misri.

Genesis 43:8

Tutainuka na kwenda ili kwamba tuishi tusife, wote sisi, wewe, na hata watoto wetu

Misemo hii "ili kwamba tuishi" pamoja na "tusife" ina maana moja. Yuda anaweka msisitizo ya kwamba wanalazimu kununua chakula Misri ili kwamba waishi. "Tutakwenda Misri na kupata nafaka ili familia yetu yote iweze kuishi"

Tutainuka

Hapa "tutainuka" ina maana ya ndugu ambao watasafiri kwenda Misri.

ili kwamba tuishi

Hapa "tuishi" ina maana ya ndugu, Israeli na familia nzima.

wote sisi

Hapa "sisi" ina maana ya hawa ndugu.

sisi, wewe

Hapa "wewe" ni umoja na ina maana ya Israeli.

na hata watoto wetu

Hapa "wetu" ina maana ya hawa ndugu. Hii ina maana ya watoto wadogo ambao wangeweza kufa katika kipindi cha njaa.

Mimi nitakuwa mdhamini wake

Nomino inayojitegemea "mdhamini" inaweza kuwekwa kama kitenzi "ahidi". "Ninaahidi kumrudisha"

Utaniwajibisha mimi

Jinsi ambavyo Yakobo atamuwajibisha Yuda inaweza kuwekwa wazi. "Utanifanya niwajibike kwako kuhusu kitakachotokea kwa Benyamini"

basi nibebe lawama

Hii inazungumzia kuhusu "lawama" kana kwamba ilikuwa kitu ambacho mtu anaweza kubeba. "Unaweza kunilaumu"

Kwani kama tusingekawia

Yuda anaelezea jambo ambalo lingetokea hapo nyuma lakini halikutokea. Yuda anamkaripia baba yake kwa kusubiri muda mrefu sana kuwatuma wanawe Misri kufuata chakula zaidi.

tungekuwa tumekwisha rudi mara ya pili

"tungekuwa tumerudi mara mbili"

Genesis 43:11

Kama ni hivyo, basi fanyeni hivi

"Iwapo huu ni uchaguzi wetu pekee, basi fanyeni"

Mchukulieni

Ilikuwa kawaida kutumia neno "chini" katika kuzungumzia safari ya Kaanani kwenda Misri.

malhamu

kitu chenye mafuta chenye harufu tamu kinachotumiwa kwa ajiliya kuponya na kulinda ngozi. "dawa"

viungo

vikolezo

jozi

karanga ndogo, itokayo kwenye mti wa kijani

lozi

karanga ya mti yenye ladha tamu

Chukueni pesa mara mbili mikononi mwenu

Hapa "mkononi" ina maana ya mtu mzima. "Chukua mara mbili ya pesa pamoja nawe"

Pesa iliyorudishwa katika magunia yenu, muichukue tena katika mikono yenu

Hapa "mikononi" ina maana ya mtu mzima. Msemo wa "iliyorudishwa" unaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "pesa iliyowekwa kwenye magunia yenu na mtu, muirudishe Misri"

Genesis 43:13

Mchukueni ndugu yenu pia

"Mchukueni pia Benyamini"

mwende tena

"mrudi"

Mungu Mwenyezi na awape kuona rehema mbele ya huyo mtu

Nomino inayojitegemea "rehema" inaweza kuwekwa kama kivumishi "huruma". "Mungu mwenye uwezo asababishe yule mtuawe na huruma kwenu"

ndugu yenu mwingine

"Simoni"

Kama nikipotelewa na watoto, nimepotelewa

"Kama nikipoteza watoto wangu, basi nipoteze watoto wangu". Hii ina maana ya kwamba Yakobo anajua inapaswa akubali kitakachotokea kwa watoto wake.

mikono yao wakachukua

Hapa "mikono" ina maana ya mtu mzima. "Wakachukua"

wakashuka Misri

Ilikuwa kawaida kutumia msemo "kushuka" pale ambapo inazungumziwa safari ya kutoka Kaanani kwenda Misri.

Genesis 43:16

Benjamini akiwa nao

"Benyamini pamoja na ndugu wa Yusufu wakubwa"

mtunzaji wa nyumba yake

"Mtunzaji" aliwajibika na kusimamia matukio ya nyumba ya Yusufu.

Akawaleta wale watu

Hapa "akawaleta" inaweza kutafsiriwa kama "kuwachukua"

nyumbani kwa Yusufu

"ndani ya nyumba ya Yusufu"

Genesis 43:18

Wale ndugu wakaogopa

"Ndugu wa Yusufu waliogopa"

walivyoletwa katika nyumba ya Yusufu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "walikwenda ndani ya nyumba ya Yusufu" au "mtunzaji aliwapeleka ndani ya nyumba ya Yusufu"

Ni kwa sababu ya pesa iliyorudishwa katika magunia yetu mara ya kwanza tulipoletwa ndani

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mtunzaji anatuleta ndani ya nyumba kwa sababu ya pesa ambayo mtu alirudisha ndani ya magunia yetu"

kwamba atafute nafasi kinyume chetu. Kwamba aweze kutukamata

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. "Anasubiria nafasi ya kutushtaki, ili kwamba aweze kutukamata"

tulikuja

Ilikuwa kawaida kutumia msemo "kushuka" pale ambapo inazungumziwa safari ya kutoka Kaanani kwenda Misri.

Genesis 43:21

Kauli Kiunganishi:

Ndugu wanaendelea kuzungumza na mtunzaji wa nyumba.

Ikawa

Msemo huu unatumika kuweka alama ya tukio muhimu la simulizi.

tulipofika katika eneo la kupumzikia

"tulipofika mahali ambapo tulikwenda kukaa usiku ule"

tazama

Neno "tazama" hapa linaonyesha ya kwamba ndugu walishangazwa kwa kile walichokiona.

pesa ya kila mtu ilikuwa katika gunia lake, pesa yetu kwa kiasi kamili

"kila mmoja wetu alikuta pesa kamili katika gunia lake"

Tumeileta katika mikono yetu.

Hapa "mikono" ina maana ya mtu mzima. "Tumerudisha pesa pamoja nasi"

Tumekuja na pesa nyingine pia mikononi mwetu ili kununua chakula

Hapa "mikono" ina maana ya mtu mzima. "Tumekuja na pesa zaidi pia kununua chakula zaidi"

Tumekuja na

Ilikuwa kawaida kutumia msemo "kushuka" pale ambapo inazungumziwa safari ya kutoka Kaanani kwenda Misri.

Amani iwe kwenu

Nomino inayojitegemea "Amani" inaweza kuwekwa kama kitenzi. "Tulia" au "Tulieni"

Mungu wenu na Mungu wa baba yenu

Mtunzaji hazungumzi kuhusu Mungu wawili tofauti. "Mungu wenu, Mungu ambaye baba yenu anamwabudu"

Genesis 43:24

wakaosha miguu yao

Utamaduni huu ulisaidia wasafiri waliochoka kujiburudisha baada ya kutembea umbali mrefu. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi.

Akawalisha punda wao

"malisho" ni chakula kilichokauka ambacho huwekwa kando kwa ajili ya wanyama.

Genesis 43:26

wakaleta nyumbani zawadi iliyokuwa mikononi mwao

Hapa "mikononi" ina maana ya mtu mzima. "ndugu hawa walileta zawadi ambazo walikuwa nazo"

wakainama mbele yake

Hii ni njia ya kuonyesha heshima na taadhima.

Genesis 43:28

Mtumishi wako baba yetu

Walimuelezea baba yao kama "Mtumishi wako" kuonyesha heshima. "Baba yetu anayekutumikia"

Wakajinyenyekeza na kuinama chini

Maneno haya yana maana moja. Walilala chini mbele ya yule mtu kumuonyesha heshima. "Waliinama chini mbele yake"

Alipoinua macho yake

Hii ina maana "alitazama juu"

mwana wa mamaye, naye akasema

Hii inaweza kutafsiriwa na sentensi mpya. "mwana wa mamaye. Yusufu akamwambia"

Je huyu ndiye mdogo wenu ... mliyemsema?

Maana zaweza kuwa 1) Yusufu anauliza kwa dhati swali kupata uthibitisho ya kwamba mtu huyu ni Benyamini, au 2) ni swali la balagha. "Kwa hiyo huyu ndiye ndugu yenu mdogo ... mliyesema?"

mwanangu

Hii ni njia ya kirafiki mtu huzungumza kwa mtu mwingine wa cheo cha chini. "kijana"

Genesis 43:30

akaharakisha kutoka chumbani

"aliharakisha nje ya chumba"

kwani aliguswa sana kuhusu nduguye

Msemo "aliguswa sana" una maana ya kuwa na huruma kubwa au hisia ambapo jambo muhimu hutokea. "kwa maana alipatwa na hisia kali za huruma kwa nduguye" au "kwa maana akawa na hisia za upendo kwa ndugu yake"

akasema

Inaweza kuwekwa wazi ni kwa nani Yusufu anazungumza. "na akasema kwa watumishi wake"

karibuni chakula

Hii ina maana ya kusambaza chakula ili kila mtu aweze kula.

Genesis 43:32

Watumishi wakamhudumia Yusufu peke yake na wale ndugu peke yao. Wamisri pale wakala pamoja naye peke yao

Hii ina maana ya kwamba Yusufu, ndugu zake, na Wamisri wengine wanakula katika sehemu tatu tofauti ndani ya chumba kimoja. "Watumishi walimhudumia Yusufu peke yake na ndugu zake peke yao na Wamisri, ambao walikuwa wakila naye, peke yao"

Wamisri pale wakala pamoja naye peke yao

Inawezekana hawa ni maafisa Wamisri wengine ambao walikula pamoja na Yusufu, lakini bado waliketi tofauti kutoka kwake na ndugu zake wa Kiebrania.

kwa sababu Wamisri hawakuweza kula mkate na Waebrania, kwani hilo ni chukizo kwa Wamisri

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. "Walifanya hivi kwa sababu Wamisri walidhani ilikuwa aibu kula pamoja na Waebrania"

hawakuweza kula mkate

Hapa "mkate" ina maana ya chakula kwa ujumla.

Wale ndugu wakakaa mbele yake

Inasemekana ya kwamba Yusufu alipanga ni wapi kila ndugu angeketi. Unaweza kuweka wazi taarifa iliyodokezwa. "Ndugu walikaa upande wa pili na yule mtu, kulingana na jinsi alivyopanga nafasi zao"

mzaliwa wa kwanza kwa kulingana na haki yake ya uzaliwa, na mdogo kulingana na ujana wake

"mzaliwa wa kwanza" na "mdogo kuliko wote" inatumika pamoja kumaanisha ya kwamba ndugu wote walikaa kulingana na umri wao.

Wale watu wakashangaa wote

"Hawa watu walishangazwa walipogundua hili"

Lakini sehemu ya Benjamini ilikuwa mara tano zaidi ya kila ndugu zake

Msemo "mara tano" unaweza kuwekwa kwa ujumla zaidi. "Lakini Benyamini alipokea sehemu ambayo ilikuwa kubwa zaidi ya kile walichopokea ndugu zake"

Genesis 44

Genesis 44:1

Maelezo ya Jumla:

Hii inaanza sehemu mpya ya tukio katika simulizi. Inawezekana hii ni asubuhi iliyofuata baada ya sherehe.

msimamizi wa nyumba yake

"msimamizi" alikuwa na wajibu wa kusimamia matukio ya nyumba ya Yusufu.

pesa ya kila mtu

Pesa yao ilikuwa sarafu za fedha yawezekana ndani ya mfuko mdogo.

katika mdomo wa gunia lake

"katika gunia lake"

Uweke kikombe changu, cha fedha

"Weka kikombe changu cha fedha"

katika mdomo wa gunia la mdogo

Neno "ndugu" linaeleweka. "ndani ya gunia la ndugu mdogo"

Genesis 44:3

Kukapambazuka asubuh

"Mwanga wa asubuhi ulionekana"

wale watu wakaruhusiwa kuondoka, wao na punda zao

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "waliwatuma watu waondoke, pamoja na punda zao"

Kwa nini mmelipa uovu badala ya mema?

Swali hili linatumiwa kukaripia wale ndugu. "Mmetutendea vibaya, baada ya sisi kuwa wema kwenu!"

Je hiki siyo kikombe ambacho bwana wangu hukinywea, na kikombe akitumiacho kwa uaguzi?

Swali hili linatumika kukaripia wale ndugu. "Tayari mnafahamu ya kwamba hiki ni kikombe ambacho bwana wangu hutumia kunywea na kwa uaguzi!"

Mmefanya vibaya, kwa jambo hili mlilolifanya.

Hii inarudia "mmefanya" kuonyesha msisitizo. "Kile mlichofanya ni kibaya sana"

Genesis 44:6

kuwambia maneno haya

Hapa "maneno" yana maana ya kile kilichosemwa. "alizungumza kile Yusufu alichomuambia kusema"

Kwa nini bwana wetu anasema maneno kama haya?

Hapa "maneno" yana maana ya kile kilichosemwa. Ndugu wanataja msimamizi kama "bwana wangu". Hii njia maalumu ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka makubwa zaidi. Inaweza kuwekwa katika lugha ya upili. "Kwa nini unasema hivi, bwana wangu?"

Na iwe mbali na watumishi wako kwamba wanaweza kufanya jambo hili

Ndugu wanajitambua wenyewe kama "watumishi wako" na "wao". Hii ni njia maalumu ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka makubwa zaidi. "Hatuwezi kufanya jambo kama hilo!"

Na iwe mbali na watumishi

Jambo ambalo mtu hawezi kufanya inazungumziwa kana kwamba ilikuwa kitu ambacho mtu anataka kukiweka mbali nacho.

Genesis 44:8

Tazama

Hii inaongeza msisitizo kwa kile ndugu wanasema baadae.

pesa tulizozikuta katika midomo ya magunia yetu

"unajua pesa ambayo tumeipata ndani ya magunia yetu"

tulizileta kwako kutoka katika nchi ya Kanaani

"tumerudisha kwako kutoka Kaanani"

Ni kwa jinsi gani basi tunaweza kuiba katika nyumba ya bwana wako fedha au dhahabu?

Ndugu wanatumia swali kuweka msisitizo ya kwamba hawawezi kuiba kutoka katika bwana wa Misri. "Kwa hiyo hatuwezi kuchukua kitu chochote kutoka kwenye nyumba ya bwana wako!"

fedha au dhahabu

Maneno haya yanatumiwa pamoja kumaanisha ya kwamba hawawezi kuiba kitu chochote chenye thamani yoyote.

Yeyote kitakayeonekana kwake miongoni mwa watumishi wako

Ndugu wanajitambua wao kama "watumishi wako". Hii njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka makubwa. Inaweza kuwekwa katika lugha ya mtu mmoja. Pia, "kitakayeonekana" linaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Ukikuta ya kwamba mmoja wetu ameiba kikombe"

nasi sote tutakuwa watumwa wa bwana wangu

Msemo "bwana wangu" una maana ya mtunzaji. Hii inaweza kuwekwa katika lugha ya upili. "Unaweza kutuchukua kama watumwa wako"

Basi na iwe kwa kadiri ya maneno yenu

Hapa "basi" haimaanishi "katika kipindi hiki" lakini inatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata. Pia "maneno" ina maana ya kile kilichosemwa. "Vizuri sana. Nitafanya kile ulichosema"

Yeye ambaye kikombe kitaonekana kwake atakuwa mtumwa wangu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Kama nikikuta kikombe ndani ya moja ya magunia yenu, mtu huyo atakuwa mtumwa wangu"

Genesis 44:11

kulishusha gunia lake chini

"akateremsha gunia lake"

mkubwa ... kwa mdogo wa wote

Neno "ndugu" linaeleweka. "ndugu mkubwa ... ndugu mdogo wa wote"

mdogo wa wote, na kikombe kikaonekana katika gunia la Benyamini

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya na katika hali ya kutenda. "mdogo wa wote. Mtunzaji alikuta kikombe ndani ya gunia la Benyamini"

Wakararua mavazi yao

Neno "wakararua" ina maana ya wale ndugu. Kurarua nguo ilikuwa ishara ya dhiki na majonzi makubwa.

nao wakarudi

"na wakarudi"

Genesis 44:14

Bado alikuwepo pale

"Yusufu alikuwa bado yupo pale"

wakainama mbele zake

"wakaanguka mbele yake". Hii ni ishara ya ndugu kutaka bwana awe na huruma kwao.

Je hamjui kwamba mtu kama mimi anafanya uaguzi

Yusufu anatumia swali kukaripia ndugu zake. "Hakika mnajua ya kwamba mtu kama mimi naweza kujifunza mambo kwa uaguzi!"

Genesis 44:16

Je tunaweza kumwambia nini bwana wangu? Tuseme nini? au ni jinsi gani twaweza kujithibitisha wenyewe?

Maswali yote 3 yana maana moja. Wanatumia maswali haya kuweka msisitizo ya kwamba hakuna kitu wanaweza kusema kuelezea kilichotokea. "Hatuna kitu cha kusema, bwana wangu. Hatuwezi kuzungumza jambo lolote la maana. Hatuwezi kujithibitisha"

Je tunaweza kumwambia nini bwana wangu ... watumwa wa bwana wangu

Hapa "bwana wangu" ina maana ya Yusufu. Hii njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka makubwa. Inaweza kuwekwa katika lugha ya mtu wa pili. "Tunaweza kusema nini kwako ... watumwa wako"

Mungu ameona uovu wa watumishi wako

Hapa "ameona" haimaanishi Mungu ameona tu kile ndugu walichofanya. Ina maana Mungu sasa anawaadhibu kwa kile walichofanya. "Mungu anatuadhibu kwa dhambi zetu za zamani"

uovu wa watumishi wako

Ndugu wanajitambulisha wenyewe kama "watumishi wako". Hii ni njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka makubwa. Inaweza kuwekwa katika lugha ya mtu wa kwanza. "dhambi zetu"

na yule ambaye kikombe kimeonekana mkononi mwake

Hapa "mkononi" ina maana ya mtu mzima. Pia, "kimeonekana" inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "na yule ambaye alikuwa na kikombe"

Na iwe mbali nami kwamba naweza kufanya hivyo

Kitu ambacho mtu hawezi kufanya inazungumziwa kana kwamba ilikuwa kitu mtu anataka kuweka mbali na yeye. "sio kawaida yangu kufanya jambo kama hili"

Mtu ambaye kikombe kimeonekana mkononi mwake

Hapa "mkononi" ina maana ya mtu mzima. Pia, "kimeonekana" inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "mtu aliyekuwa na kikombe changu"

Genesis 44:18

alipomkaribia

"akakaribia"

mwache mtumishi wako

Yuda anajitambulisha kama "mtumishi wako". Hii ni njia rasmi ya kuzungumza kwa mtu mwenye mamlaka zaidi. Hii inaweza kuwekwa katika lugha ya mtu wa kwanza. "niruhusu mimi, mtumishi wako"

aseme neno katika masikio ya bwana wangu

Hapa "neno" ni lugha nyingine yenye maana ya kile kilichosemwa. Na "masikio" ni lugha nyingine yenye maana ya mtu mzima. "kuzungumza na wewe, bwana wangu"

masikio ya bwana wangu

Hapa "bwana wangu" ina maana ya Yusufu. Hii ni njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka zaidi. Hii inaweza kuwekwa katika lugha ya mtu wa pili. "kwako"

na usiziache hasira zako kuwaka dhidi ya mtumishi wako

Kuwa na hasira inazungumzwa kana kwamba ilikuwa moto unawaka. "tafadhali usiwe na hasira na mimi, mtumishi wako"

kwani wewe ni kama Farao

Yuda anamlinganisha bwana yule na Farao kusisitiza nguvu kubwa ambayo bwana yule alikuwa naye. Pia anadokeza ya kwamba hakutaka bwana kuwa na hasira na kumuadhibu. "kwa maana wewe kama Farao mwenye mamlaka na unaweza kuwaamuru askari wako kuniua"

Bwana wangu aliwauliza watumishi wake, kusema, Je mnaye baba au ndugu?'

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Bwana wangu alituuliza kama tuna baba na ndugu"

Bwana wangu aliwauliza watumishi wake

Yuda anamtambua Yusufu kwa maneno haya "bwana wangu" na "wake". Pia anajitambulisha mwenyewe na ndugu zake kama "watumishi wake". "Wewe, bwana wangu, alituuliza, watumishi wako" au "Ulituuliza"

Genesis 44:20

Maelezo ya Jumla:

Yuda anaendelea kuzungumza mbele ya Yusufu.

Nasi tukamwambia bwana wangu, 'Tunaye baba ... baba yake anampenda.'

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Nasi tukamwambia bwana wetu ya kwamba tuna baba ... baba yake anampenda"

tukamwambia bwana wangu

Yuda anamtambua Yusufu kama "bwan wangu". Hii ni njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka makubwa. "tulisema kwako, bwana wangu"

baba yake anampenda

Hii ina maana ya upendo kwa rafiki au mmoja wa familia.

Nawe ukawambia watumishi wako, 'Mleteni ili nimwone.'

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Nawe ukasema kwa mtumishi wako ya kwamba tunapaswa kumleta ndugu yetu mdogo kwako ili uweze kumuona"

Nawe ukawambia watumishi wako

Yuda anajitambulisha mwenyewe na ndugu zake kama "watumishi wako". "Kisha ulisema kwetu, watumishi wako"

Mleteni ili nimwone

Ilikuwa kawaida kutumia neno "chini" pale ilipozungumziwa safari ya kutoka Kanaani kwenda Misri. "Mleteni kwangu"

Baada ya hapo, tukamwambia bwana wangu, 'Kijana hawezi ... baba yake angekufa.'

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Kwa kujibu, tulisema kwa bwana wangu ya kwamba kijana hawezi ... baba yake angekufa"

baba yake angekufa

Inadokezwa ya kwamba baba yao angekufa kwa huzuni.

Genesis 44:23

Maelezoya jumla:

Yuda anaendelea simulizi yake kuhusu Yusufu.

Na ukawambia watumishi wako, 'Mdogo wenu asipokuja pamoja nanyi, hamtauona uso wangu tena.'

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Kisha ulisema kwa watumishi wako ya kwamba hadi pale ndugu yetu mdogo aje pamoja nasi, hatutaweza kukuona tena"

Na ukawaambia watumishi wako

Yuda anajitambulisha mwenyewe na ndugu zake kama "watumishi wako". Hii ni njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka zaidi. "Kisha ukasema kwetu, watumishi wako"

asipokuja ... kushuka

Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "kushuka" kuzungumzia safari ya Kaanani kwenda Misri.

hamtauona uso wangu tena

Hapa "uso" ina maana ya mtu mzima. "Hamtaniona tena"

Ikawa

Msemo huu unatumika kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

tulipokwenda kwa mtumishi wako baba yangu

Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "kwenda" kuzungumzia safari kutoka Misri kwenda Kaanani.

tulimwambia maneno ya bwana wangu

Yuda anamtambua Yusufu kama "bwana wangu". Pia "maneno" yana maana ya kile kilichosemwa. "tulimwambia ulichosema, bwana wangu"

Na baba yetu akasema, Nendeni tena, mkatununulie chakula

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Baba yetu alituambia kurudi tena Misri kununua chakula kwa ajili yetu na familia zetu"

Nasi tukasema, "Hatuwezi kushuka. Ikiwa mdogo wetu ... pamoja nasi,

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Kisha tukamwambia ya kwamba hatuwezi kushuka Misri. Tulimwambia ya kwamba iwapo ndugu yetu mdogo atakuwa pamoja nasi ... pamoja nasi"

kuuona uso wa mtu

Hapa "uso" ina maana ya mtu mzima. "kumuona yule mtu"

Genesis 44:27

Maelezo ya Jumla:

Yuda anaendeleza simulizi yake kwa Yusufu

akatuambia, 'Mnajua kwamba mke wangu alinizalia wana wawili. Na mmoja akatoka kwangu nami nikasema, "Bila shaka ameraruliwa vipande, na tangu hapo sijamwona." Nanyi mkimchukua huyu naye kutoka kwangu mabaya yanaweza kumpata, mtashusha mvi zangu kwa kaburini kwa huzuni.

Hii ina madaraja mawili na daraja la tatu la nukuu. Yanaweza kuwekwa kama nukuu zisikzokuwa moja kwa moja. "akatuambia ya kwamba tunafahamu ya kuwa mke wake, Raheli, alimzalia watoto wawili tu, na kwamba mmoja wao alitoweka na mnyama alimrarua vipande vipande, na hajamuona tangu siku hiyo, kisha tutamfanya afe kwa huzuni"

akatuambia

Hapa "akatuambia" haimjumlishi Yusufu.

Mnajua

Hapa "mnajua" ni wingi na ina maana ya wale ndugu.

ameraruliwa vipande

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "mnyama pori alimrarua vipande vipande"

mabaya yanaweza kumpata

Jambo baya linalotokea kwa mtu inazungumziwa kana kwamba "baya" lilikuwa kitu ambacho husafiri na kuja kwa mtu.

mtashusha mvi zangu kwa kaburini kwa huzuni

"kushusha ... Kuzimu" ni njia ya kusema watasababisha afariki na kushuka Kuzimu. Anatumia neno "shuka" kwa sababu iliaminika Kuzimu ilikuwa sehemu ya chini. "kisha mtanisababisha, mtu mzee, kufa kwa huzuni"

mvi zangu

Hii ina maana ya Yakobo na inasisitiza umri wake mkubwa. "mimi, mtu mzee"

Genesis 44:30

Kwa hiyo

Hii haimaanishi "katika kipindi hiki" lakini inatumika hapa kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.

basi, nitapokuja ... huzuni ya kuzimu

Yuda anaelezea kwa Yusufu suala la ukweli lakini la kubuni ambalo linatarajiwa kutokea kwa Yakobo atakaporudi bila Benyamini.

nitapokuja kwa mtumishi wako

Hapa "nitakapokuja" inaweza kutafsiriwa kama "kwenda" au "kurudi".

kijana hayupo nasi

"kijana hayupo pamoja nasi"

kwa kuwa uhai wake umefungamanishwa katika uhai wa kijana

Baba anasema ya kwamba atakufa iwapo mwanawe atangekufa inazungumziwa kana kwamba maisha yao mawili yaliunganishwa pamoja kimwili. "kwa maana alisema angekufa iwapo kijana hangerudi"

itakuwa

Yuda anazungumzia kuhusu suala la kubuni katika wakati wa mbele kana kwamba ingetokea kweli.

watumishi wako watazishusha mvi za mtumishi wako baba yetu kaburini kwa masikitiko

"watazishusha ... Kuzimu" ni njia ya kusema watasababisha afariki na kushuka Kuzimu. Anatumia neno "shuka" kwa sababu iliaminika Kuzimu ilikuwa sehemu ya chini. "kisha mtanisababisha, mtu mzee, kufa kwa huzuni"

watumishi wako

Yuda anajitambulisha mwenyewe na ndugu zake kama "watumishi wako". Hii ni njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka zaidi. "Nasi, watumishi wako" au " Na sisi"

mvi za mtumishi wako baba yetu

Hapa "mvi" ina maana ya Yakobo na inasisitiza umri wake mkubwa. "baba yetu mzee"

Kwani mtumishi wako alikuwa mdhamini wa kijana kwa baba yangu

Nomino hii inayojitegemea "mdhamini" inaweza kuwekwa kama kitenzi "aliahidi". "Maana nimuahidi baba yangu kuhusu kijana huyu"

Kwani mtumishi wako

Yuda anajitambulisha kama "mtumishi wako". "Kwa maana mimi, mtumishi wako" au "Kwa maana mimi"

ndipo nitakapokuwa mwenye hatia kwa baba yangu

Kuchukuliwa mwenye hatia inazungumziwa kana kwamba "hatia" ilikuwa kitu ambacho mtu hubeba. "kisha baba yangu anaweza kunilaumu"

Genesis 44:33

sasa

Hii haimaanishi "katika kipindi hiki" lakini inatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.

mwache mtumishi wako

Yuda anajitambulisha mwenyewe kama "mtumishi wako". Hii ni njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka makubwa. "niruhusu mimi, mtumishi wako" au "niruhusu mimi"

kwa bwana wangu

Yuda anamtambua Yusufu kama "bwana wangu". "kwako, bwana wangu" au "kwako"

umwache kijana aende juu

Alikuwa akienda kutumia msemo wa "aende juu" pale alipozungumzia safari ya kutoka Misri kwenda Kaanani.

Kwa maana nitakwenda jinsi gani kwa baba yangu ikiwa kijana hayupo nami?

Yuda anatumia swali kuweka msisitizo wa majonzi ambayo angeyapata iwapo Benyamini asingerudi nyumbani. "Siwezi kurudi kwa baba yangu iwapo kijana hatakuwa pamoja nami"

Ninaogopa kuona mabaya yatakayompata baba yangu

Mtu anayeteseka vibaya inazungumziwa kana kwamba "uovu" ilikuwa kitu kinachokuja juu ya mtu. "Ninaogopa kumuona jinsi baba yangu atakavyoteseka"

Genesis 45

Genesis 45:1

hakuweza kujizuia mwenyewe

Hii ina maana hakuweza kuzuia hisia zake. Inaweza kuwekwa katika hali ya chanya. "alikuwa akitaka kuanza kulia"

kando yake

"karibu naye"

nyumba ya Farao

Hapa "nyumba" ina maana ya watu katika kasri ya Farao. "kila mtu ndani ya kasri ya Farao"

walitishwa na uwepo wake

"walimuogopa"

Genesis 45:4

mliyemwuza Misri

Maana inaweza kuwekwa wazi zaidi. "ambaye mlimuuza kama mtumwa kwa wafanyabiashara walionileta huku Misri"

msihuzunike

"msihuzunike" au "msiteseke"

mliniuza huku

Maana inaweza kuwekwa wazi zaidi. "ya kwamba mliniuza kama mtumwa na kunituma huku Misri"

kutunza uhai

Hapa "uhai" ina maana ya watu ambao Yusufu aliwaokoa na kifo wakati wa njaa. "Ili niweze kuokoa maisha ya wengi"

bado kuna miaka mitano ambayo hakutakuwa na kulima wala kuvuna.

"kutakuwa na miaka mitano zaidi bila ya kupanda au kuvuna". Hapa "bila ya kupanda au kuvuna" ina maana ya ukweli kwamba mimea haitaota kwa sababu ya ukame. "na njaa itadumu kwa miaka mitano zaidi"

Genesis 45:7

kuwahifadhi kama masalia duniani

"ili kwamba wewe na familia yenu msipotee kutoka duniani" au "kuhakikisha vizazi vyako vinaendelea kuishi"

kuwaweka hai kwa ukombozi mkuu

Nomino inayojitegemea "ukombozi" inaweza kuwekwa kama "kuokoa". "kukuweka hai kwa kuwaokoa kwa njia ya juu"

amenifanya baba kwa Farao

Yusufu kumshauri na kumsaidia Farao inazungumziwa kana kwamba Yusufu alikuwa baba wa Farao. "amenifanya niwe kiongozi kwa Farao" au "amenifanya kuwa mshauri mkuu kwa Farao"

nyumba yake yote

Hapa "nyumba" ina maana ya watu wanaoishi ndani ya kasri yake. "miongoni mwa nyumba yake yote" au "kati ya wote wa kasri yake"

mtawala wa nchi yote ya Misri

Hapa "nchi" ina maana ya watu. "mtawala juu ya watu wote wa Misri"

mtawala

Hapa Yusufu anamanisha ya kwamba yeye ni mtawala katika nafasi ya pili kutoka kwa Farao, mfalme wa Misri. Taarifa hii inayoeleweka inaweza kuwekwa wazi.

Genesis 45:9

mwende kwa baba yangu

Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "kushuka" kuzungumzia safari ya Kaanani kwenda Misri. "kurudi kwa baba yangu"

mmwambie, 'Hivi ndivyo asemavyo Yusufu mwanao, "Mungu amenifanya ... yote uliyonayo

Hii ni nukuu yenye madaraja matatu. Inaweza kurahisishwa katika madaraja mawili. "muambieni ya kwamba hivi ndivyo nilivyosema: "Mungu amenifanya ... yote uliyonayo"

Shuka kwangu

Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "shuka" kuzungumzia safari ya kutoka Kaanani kwenda Misri. "Njooni hapa kwangu"

ukaingia katika uhitaji

Hii inazungumzia kuhusu "uhitaji" kana kwamba ilikuwa kikomo cha safari. "kupotea bure" au "kushinda njaa"

Genesis 45:12

macho yenu yanaona, na macho ya Benjamini ndugu yangu

Neno "macho" ina maana ya mtu mzima. "Nyie wote na Benyamini mnaweza kuona"

kwamba ni kinywa changu kinachoongea nanyi

Neno "kinywa" ina maana ya mtu mzima. "ya kwamba mimi, Yusufu, nazungumza na nyinyi"

juu ya heshima yangu yote huku Misri

"jinsi watu wa Misri wanavyoniheshimu sana"

baba yangu huku chini

Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "shuka" kuzungumzia safari ya kutoka Kaanani kwenda Misri. "baba yangu huku kwangu"

Genesis 45:14

Akaikumbatia shingo ya Benjamini ndugu yake na kulia, na Benjamini akalia shingoni mwake

"Yusufu alimkumbatia ndugu yake Benyamini, na wote wakalia"

Akawabusu ndugu zake wote

Katika kipindi cha zamani cha Mashariki ya Karibu, ilikuwa kawaida kumsalimia jamaa kwa busu.

kulia kwa ajili yao

Hii ina maana ya Yusufu alilia alipowabusu.

Baada ya hayo ndugu zake wakaongea naye

Awali walikuwa na hofu juu yake. Sasa walijisikia wanaweza kuongea naye kwa uhuru. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "Baada ya hapo ndugu zake waliongea naye kwa uhuru"

Genesis 45:16

Habari ya jambo hili ikasemwa katika nyumba ya Farao: "Ndugu zake Yusufu wamekuja"

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. Pia hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Kila mtu katika kasri ya Farao alisikia ya kwamba ndugu zake Yusufu walikuja"

nyumba ya Farao

Hii ina maana ya kasri ya Farao

Wambie ndugu zako, 'Fanyeni hivi: Wapakieni wanyama wenu na mwende katika nchi ya Kanaani. Mchukueni baba yenu na nyumba zenu mnijie. Nami nitawapa mema ya nchi ya Misri, nanyi mtakula unono wa nchi.'

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Waambie ndugu zako kupakiza wanyama wao na kwenda Kaanani kumfuata baba yao na familia zao. Waambie waje hapa, nami nitawapa ardhi nzuri katika Misri na chakula bora tunachoweza kutoa"

nitawapa mema ya nchi ya Misri

"Nitawapa sehemu bora ya nchi ya Misri"

mtakula unono wa nchi

Chakula bora ambacho nchi huzaa inazungumziwa kana kwamba ilikuwa ni sehemu nene ya nchi. "utakula chakula bora katika nchi"

Genesis 45:19

Maelezo ya Jumla

Farao anaendelea kumwambia Yusufu kipi cha kuwaambia ndugu zake.

Basi

Hii haimaanishi "katika kipindi hiki" lakini inatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.

mmeamriwa, 'Fanyeni hivi, chukueni mikokoteni kutoka Misri kwa ajili ya watoto wenu na kwa ajili ya wake zenu. Mchukueni baba yenu na kuja. Msijari kuhusu mali zenu, kwani mema yote ya nchi ya Misri ni yenu

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "pia waambie kuchukua mikokoteni kutoka katika nchi ya Misri kwa ajili ya watoto na wake zao, na kumchukua baba yao aje hapa. Hawatakiwi kuwa na wasiwasi kuhusu kuleta mali zao, kwa maana nitawapatia mambo mazuri tuliyonayo ndani ya Misri"

mmeamriwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Nami nakuamuru kuwaambia" au "pia waambie"

chukueni mikokoteni

"Mikokoteni" ni gari dogo la abiria na mizigo lenye magurudumu mawili au manne. Wanyama huvuta mikokoteni.

Genesis 45:21

na akawapa mahitaji ya safari

"na kuwapa walichohitaji kwa ajili ya safari yao"

Akawapa wote mavazi ya kubadilisha

Kila mtu alipokea idadi ya nguo mbili isipokuwa kwa Benyamini aliyepokea idadi ya nguo tano.

vipande mia tatu

"vipande 300"

punda kumi ... punda majike kumi

Punda walijumlishwa kama sehemu ya zawadi.

Genesis 45:24

msijemkagombana

Maana zaweza kuwa 1) "msibishane" na 2) "msiwe na hofu"

Wakapanda kutoka Misri

Ilikuwa kawaida kutumia neno "panda" kuzungumzia safari ya kutoka Misri kwenda Kaanani.

ndiye mtawala juu ya nchi yote ya Misri

Hapa "nchi ya Misri" ina maana ya watu wa Misri. "anatawala watu wote wa Misri"

moyo wake ulishikwa na mshangao

Hapa "moyo" ina maana ya mtu mzima. "na alishtuka" au "na alishangazwa sana"

hakuwaamini walichomuambia

"hakupokea kile walichosema kilikuwa ni cha kweli"

Genesis 45:27

Wakamwambia

"Wakamwambia Yakobo"

maneno yote ya Yusufu aliyokuwa amewaambia

Hapa "maneno" yana maana ya kile kilichosemwa. "kila kitu ambacho Yusufu alikisema kwao"

roho ya Yakobo baba yao ikafufuka

Neno la "roho" lina maana ya mtu mzima. "Yakobo baba yao alipona" au "Yakobo baba yao akawa na furaha sana"

Genesis 46

Genesis 46:1

akaja Beersheba

"alikuja Beersheba"

Mimi hapa

"Ndio, ninasikiliza"

kushuka Misri

Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "shuka" kuzungumzia safari ya kutoka Kaanani kwenda Misri.

nitakufanya taifa kubwa

Hapa "nitakufanya" ni katika umoja na una maana ya Yakobo. Hii "nitakufanya" pia ina maana ya uzao wa Israeli ambao watakuwa taifa kubwa. "Nitakupatia uzao mkubwa, nao watakuwa taifa kubwa"

huko Misri

"huko Misri"

Nami nitakupandisha huku tena bila shaka

Ahadi ilifanywa kwa Yakobo, lakini ahadi hii ingetimizwa kwa uzao wote wa Yakobo. "Hakika nitaleta uzao wako kutoka Misri tena"

nitakupandisha huku tena

Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "kupanda" kuzungumzia safari ya kutoka Misri kwenda Kaanani.

Na Yusufu akayafunika macho yako kwa mikono yake

Msemo huu "akayafunika macho yako kwa mikono yake" ni njia ya kusema ya kwamba Yusufu atakuwepo pale ambapo Israeli atakufa na Yusufu atauafumba macho ya Yakobo katika kipindi cha kifo chake. "Na Yusufu pia atakuwepo pamoja na wewe katika kipindi cha kifo chako"

akayafunika macho yako

Ilikuwa ni utamaduni kufunika kope za macho pale mtu anapokufa na macho yake wazi. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi.

Genesis 46:5

akainuka kutoka

"kuwekwa kutoka kwa"

katika mikokoteni

"Mikokoteni" ni gari dogo la abiria na mizigo lenye magurudumu mawili au manne. Wanyama huvuta mikokoteni.

walizokuwa wamezipata

"ambazo walikusanya" au "waliopata"

Akaja pamoja nao

"Yakobo akaja pamoja nao"

wanawe

"wajukuu wake"

wana wa binti zake

"wajukuu wake wa kike"

Genesis 46:8

Haya ni majina

Hii ina maana ya majina ya watu ambao mwandishi anataka kuwaorodhesha.

ya watoto wa Israeli

"ya watoto wa familia ya Israeli"

Hanoki na Palu na Hezroni na Karmi ... Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Zohari, na Shauli ... Gershoni, Kohathi, na Merari

Haya ni majina ya wanamume.

Genesis 46:12

Eri, Onani, Shela

Hawa walikuwa wana wa Yuda kwa mke wake, Shua.

Shela na Zera

Hawa walikuwa wana wa Yuda kwa mkwe wake, Tamari.

Hezroni ... Hamuli ... Tola, Puva, Lobu ... Shimroni ... Seredi, Eloni ... Yahleeli

Haya ni majina ya wanamume.

Dina

Hili ni jina la binti wa Lea.

Wanawe na binti zake walikuwa thelathini na watatu

watatu - Hapa "wanawe" na "mabinti" ina maana ya wana wa Yakobo, mabinti , na wajukuu wenye uhusuiano na Lea. "Kwa pamoja alikuwa na watoto 33, mabinti na wajukuu"

Genesis 46:16

Zifioni ... Hagi, Shuni ... Ezboni, Eri, Arodi ... Areli ... Imna ... Ishva, Ishvi ... Beria ... Heberi ... Malkieli

Haya ni majina ya wanamume.

Sera

Hili ni jina la mwanamke

Zilpa

Hili ni jina la mtumishi wa kike wa Lea.

Wana hawa aliomzalia Yakobo - kumi na sita kwa ujumla

Hii ina maana ya watoto 16, wajukuu, na watukuu ambao walikuwa na uhusiano na Zilpa.

Genesis 46:19

Asenathi

"Asenathi" ni jina la mwanamke ambaye Farao alimpa Yusufu kuwa mke wake.

Potifera

"Potifera" ni baba yake Asenathi.

kuhani wa Oni

Oni ni mji, ambao pia unajulikana kama Heliopolisi, ambao ulikuwa "Mji wa Jua" na makao ya kumuabudu mungu wa jua Ra.

Bela, Bekeri, Ashbeli, Gera, Naamani, Ehi, Roshi, Mupimu, Hupimu, na Ardi

Haya ni majina ya wanamume.

jumla yao kumi na wanne

Hii ina maana ya wana 14 na wajukuu waliokuwa wamehusiana na Raheli.

Genesis 46:23

Hushimu ... Yahzeeli, Guni, Yezeri ... Shilemi

Haya ni majina ya wanamume.

Bilha

Hili ni jina la mtumishi wa kike wa Raheli.

wote walikuwa saba

Hii ina maana ya wana 7 na wajukuu waliokuwa wamehusiana na Bilha.

Genesis 46:26

sitini na sita

sita - "66"

sabini

"70"

Genesis 46:28

kuonesha njia mbele yake kwenda Gosheni

"kuwaonyesha njia ya kuelekea Gosheni"

Yusufu akaandaa kibandawazi chake na akaenda

Hapa "Yusufu" ina maana ya watumishi wake. "Watumishi wa Yusufu waliaanda kibandawazi chake na Yusufu akenda juu"

akaenda kukutana na baba yake Israeli

Msemo wa "kwenda juu" unatumika kwa sababu Yusufu anasafiri kwenye kwenye mwinuko kukutana na baba yake" "akaenda kukutana na baba yake"

akaikumbatia shingo yake, na akalia shingoni mwake kwa muda mrefu

"akaweka mikono yake kumzunguka baba yake, na kulia kwa muda mrefu"

Basi na nife sasa

"Sasa nipo tayari kufa" au "Sasa nitakufa na furaha"

kwa kuwa nimeuona uso wako, kwamba bado uko hai

Hapa "uso" ina maana ya mtu mzima. Yakobo anaonyesha furaha ya kumuona Yusufu. "kwa maana nimekuona ukiwa hai tena"

Genesis 46:31

nyumba ya baba yake

Hapa "nyumba" ina maana ya familia yake. "familia ya baba yake" au "nyumba ya baba yake"

Nitakwenda na kumwambia Farao

Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "kwenda juu" pale mtu azungumzapo na mtu mwenye mamlaka makubwa. "Nitakwenda kumwambia Farao"

kumwambia Farao, kusema, 'Ndugu zangu ... vyote walivyonavyo.'

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "mwambie Farao ya kwamba ndugu zangu ... vyote walivyonavyo"

Genesis 46:33

Itakuwa

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama kwa tukio muhimu ambalo linataka kutokea katika simulizi.

na kuwauliza, 'Kazi yenu ni ipi?' mwambieni,

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "mwambieni, 'Watumishi wako wamekuwa ... sisi, na baba zetu."

mwambieni, 'Watumishi wako wamekuwa ...sisi, na baba zetu."

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "mwambieni, 'Watumishi wako wamekuwa ... sisi, na baba zetu."

Watumishi wako

Familia ya Yusufu wanajitambulisha kama "watumishi wako" wanapozungumza na Farao. Hii ni njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka makubwa. Inaweza kuwekwa katika lugha ya mtu wa kwanza. "Sisi, watumishi wako"

kila mfugaji ni chukizo kwa Wamisri

Nomino inayojitegemea ya "chukizo" inaweza kutafsiriwa na kivumishi "yenye maudhi". "Wamisri wanadhani ufugaji ni maudhi"

Genesis 47

Genesis 47:1

Akawachukua watano katika ndugu zake

tafsiri inaorodhesha tukio pamoja na Farao katika mpangilio, wakati tafsiri zingine huorodhesha matukio kama mwandishi alivyoandika.

Genesis 47:3

Watumishi wako ni wafugaji

"Watumishi wako wanafuga mifugo"

Watumishi wako

Ndugu wa Yusufu wanajitambua kama "watumishi wako". Hii ni njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka makubwa zaidi. Hii inaweza katika lugha ya mtu wa kwanza. "Sisi, watumishi wako" au "Sisi"

kama mababu zetu

"wote sisi na baba zetu" au "wote sisi na mababu zetu"

Tumekuja kukaa kwa muda katika nchi

"Tumekuja kukaa kwa muda mfupi Misri"

Hakuna malisho

"Hakuna nyasi ya kula"

Hivyo

Hii haimaanishi "katika kipindi hiki" lakini inatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.

Genesis 47:5

Nchi ya Misri iko mbele yako

"Nchi ya Misri ipo wazi kwako" au "Nchi yote ya Misri ipo wazi kwako"

Mkalishe baba yako na ndugu zako katika eneo zuri, nchi ya Gosheni

"Muweke baba yako na ndugu zako katika nchi ya Gosheni, ambayo ni sehemu bora zaidi"

Ikiwa unafahamu watu wenye uwezo miongoni mwao

Inasemekana ya kwamba walikuwa na uwezo wa kuchunga wanyama. "Kama unawajua wanamume wowote miongoni mwao wenye uwezo wa kutunza mifugo"

Genesis 47:7

Yakobo akambariki Farao

Hapa "kubarikiwa" ina maana ya kuonyesha hamu ya mambo chanya na yenye manufaa kutokea kwa mtu huyo.

Umeishi kwa muda gani?

"Una umri gani?"

Miaka ya safari zangu ni mia moja na thelathini

Msemo wa "miaka ya safari zangu" ina maana ya muda ambao aliishi duniani akisafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine. "Nimesafiri duniani kwa miaka 130"

Miaka ya maisha yangu imekuwa mifupi ... Siyo kama miaka ya baba zangu.

Yakobo ina maana ya kwamba maisha yake ni mafupi kulinganisha na maisha ya Abrahamu na Isaka.

na ya maumivu

Yakobo ameonyesha maumivu mengi na matatizo wakati wa maisha yake.

Genesis 47:11

Kisha Yusufu akamweka baba yake na ndugu zake

"Kisha Yusufu akamweka baba yake na ndugu zake na kuwasaidia kuimarisha sehemu watakapoishi"

eneo la Ramesesi

Hili ni jina la nchi ya Gosheni.

kulingana na hesabu ya wahitaji wao

Hapa, neno "wahitaji" lina maana ya watoto wadogo katika familia. "kulingana na idadi ya watoto wadogo ndani ya familia zao"

Genesis 47:13

Basi

Neno hili linatumika hapa kuweka alama ya pumziko katika zimulizi kuu. Hapa mwandishi anaanza kuelezea sehemu mpya ya simulizi.

Nchi ya Misri na nchi ya Kanaani

Hii ina maana ya watu wanaoishi katika nchi hizi. "watu wa Misri na watu wa Kaanani"

ikaharibika

"ikawa nyembamba na dhaifu"

Yusufu akakusanya pesa yote iliyokuwa katika nchi ya Misri na nchi ya Kanaani, kwa kuwauzia wakaaji wake nafaka

"Watu wa Misri na Kaanani walitumia pesa yao kununua nafaka kutoka kwa Yusufu"

Yusufu akakusanya ... Yusufu akaleta

Inawezekana Yusufu aliwaamuru watumishi wake kukusanya na kuleta ile pesa"

Genesis 47:15

Pesa yote ya nchi za Misri na Kanaani ilipokwisha

Hapa "nchi" ina maana ya watu wanaoishi katika nchi zile. Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "Pale ambapo watu wa Misri na Kaanani watakapomaliza pesa yao yote"

ya nchi za Misri na Kanaani

"kutoka katika nchi ya Misri na kutoka katika nchi ya Kaanani"

Kwa nini tufe mbele zako kwa maana pesa yetu imekwisha?

Watu walitumia swali kuweka msisitizo jinsi gani walivyokuwa na haja ya kununua chakula kutokana na kukata tamaa. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Tafadhali, usituruhusu tufe kwa sababu tumetumia pesa yetu yote!"

Akawalisha kwa mkate

Hapa "mkate" una maana ya chakula kwa ujumla. "Aliwapatia chakula" au "Aliwagawia chakula"

Genesis 47:18

wakaja kwake

"watu wakaja kwa Yusufu"

Hatutaficha kwa bwana wangu

Watu wanamtambua Yusufu kama "bwana wangu". Hii ni njia rasmi ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka makubwa. Inaweza kuwekwa katika lugha ya mtu wa pili. "Hatutajificha kwako, bwana wetu" au "Hatutajificka kutoka kwako"

Hakuna kilichobaki machoni pa bwana wangu

Hapa "machoni" ina maana ya Yusufu mwenyewe. "Hatuna kitu kilichobaki kukupa, bwana wetu"

Kwa nini tufe mbele za macho yake, sisi na nchi yetu?

Neno la "macho" lina maana ya macho ya Yusufu. Watu hutumia swali kuweka msisitizo jinsi walivyo na hamu ya kununua chakula. swali hili linaweza kutasfiriwa kama kauli. "Tafadhali usitazame tu tunavyokufa na nchi yetu inaharibika!"

Kwa nini tufe ... wote sisi na nchi yetu?

Nchi inakuwa haina faida na inaharibika kwa sababu hakuna mbegu ya kupanda; kwa hiyo inazungumziwa kana kwamba nchi itakufa.

Genesis 47:20

Kwa njia hii, nchi ikawa mali ya Farao

"Kwa hiyo nchi ikawa ya Farao"

Ilikuwa ni nchi ya makuhani pekee ambayo Yusufu hakuinunua

"Lakini hakununua nchi ya makuhani"

makuhani walikuwa wakipewa posho

"Posho" ni kiasi cha pesa au chakula ambacho mtu hutoa mara kwa mara mtu mwingine. Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "Farao aliwapa makuhani kiasi fulani cha chakula kila siku"

Walikula katika sehemu aliyowapa Farao

"Walikula kutoka kwa kile ambacho Farao aliwapatia"

Genesis 47:23

nanyi mtapanda

"ili muweze kupanda"

Wakati wa mavuno, mtampa Farao sehemu ya tano, na sehemu nne zitakuwa zenu

Neno la "tano" ni sehemu. "Wakati wa mavuno utagawanyisha mazao katika sehemu tano. Utatoa sehemu moja kwa Farao kwa ajili ya malipo na sehemu nne ni kwa ajili yenu"

wa chakula cha nyumba zenu na watoto wenu

Unaweza kuwekwa wazi taarifa inayoeleweka. "kwa chakula kwa ajili ya nyumba zenu na kwa chakula kwa ajili ya watoto wenu"

Genesis 47:25

Na tupate kibali machoni pako

Hapa "macho" ina maana ya fikra na mawazo. "Na ufurahishwe na sisi"

tupate kibali

Hii ina maana ya kwamba mtu anakubalika kwa mtu mwingine.

katika nchi ya Misri

"katika nchi ya Misri" au "katika nchi yote ya Misri"

hata leo

Hii ina maana katika kipindi ambacho mwandishi alikuwa akiandika haya.

moja ya tano

tano- Neno la "tano" ni sehemu. "Wakati wa mavuno utagawanyisha mazao katika sehemu tano. Utatoa sehemu moja kwa Farao kwa ajili ya malipo na sehemu nne ni kwa ajili yenu"

Genesis 47:27

Walikuwa wenye kuzaa na kuongezeka sana

Neno "kuongezeka" linaelezea jinsi walivyokuwa "wamezaana". "Walikuwa na watoto wengi sana"

Walikuwa wenye kuzaa

Hapa "kuzaa" ina maana ya kufanikiwa au kupata watoto.

miaka kumi na saba

"miaka 17"

kwa hiyo miaka ya maisha ya Yakobo ilikuwa miaka mia moja arobaini na saba

miaka saba - "kwa hiyo Yakobo aliishi hadi umri wa miaka 147"

Genesis 47:29

Wakati wa kufa kwake Yakobo ulipokaribia

Hii inazungumzia juu ya muda kana kwamba inasafiri na kutua mahali. "Muda wa Israeli kufariki ulipokaribia"

Ikiwa nimepata kibali machoni pako

Hapa "machoni" ina maana ya fikra na mawazo. "Kama nimepata kibali na wewe" au "Kama nimekufurahisha"

sasa

Hii haimaanishi "katika kipindi hiki" lakini inatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.

nimepata kibali

Hii ina maana ya kwamba mtu amekubalika na mtu mwingine.

weka mkono wako chini ya paja langu

Tendo hili ni ishara ya kufanya ahadi ya dhati.

unionyeshe uaminifu na kweli

Nomino inayojitegemea ya "uaminifu"na "kweli" zinaweza kutafsiriwa kama vivumishi. "nitendee kwa namna ya uaminifu na kweli"

Tafadhari usinizike Misri

Neno "tafadhali" linaongeza msisitizo kwa ombi lake.

Nitakapolala na baba zangu

Hapa "kulala" ni njia ya upole ya kumaanisha kufa. "Nitakapokufa na kujiunga na wa familia yangu waliokufa kabla yangu"

Niapie

"Niahidi" au "Fanya kiapo kwangu"

akamwapia

"allimuahidi" au "alifanya kiapo kwake"

Genesis 48

Genesis 48:1

Ikawa

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

mmojawapo akamwambia Yusufu

"mtu akamwambia Yusufu"

Tazama, baba yako

"Sikiliza, baba yako". Hapa neno "tazama" linatumika kuvuta nadhari ya Yusufu.

Hivyo akaondoka

"Kwa hiyo Yusufu akaondoka"

Yakobo alipoambiwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mtu alipomuambia Yakobo"

mwanao Yusufu amekuja kukuona

"mwanao Yusufu amekuja kwako"

Israeli akakusanya nguvu na kukaa juu ya kitanda

Hapa mwandishi anazungumzia juu ya Israeli kuhangaika kuketi kitandani kana kwamba alikuwa akikusanya "nguvu" kama vile mtu akusanyavyo vitu halisia. "Israeli alifanya bidii kubwa kukaa kitandani" au "Israeli alihangaika alipokaa juu kitandani"

Genesis 48:3

Luzu

Hili ni jina la mji.

katika nchi ya Kanaani. Akanibariki na kuniambia

Hii inaweza kutafsiriwa kwa sentensi mpya ikianzia katika sehemu mpya. "katika nchi ya Kaanani, na akanibariki. Na akasema kwangu"

akanibariki

Hii ina maana ya Mungu kutamka baraka rasmi kwa mtu.

na kuniambia, 'Tazama, nitakupa uzao mwingi, na kukuzidisha. Nitakufanya kuwa kusanyiko la mataifa. Nitakupa nchi hii wewe na uzao wako kuwa milki ya milele

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "na kusema kwangu ya kwamba angenifanya niwe na uzao mwingi na kunizidishia. Na akasema ya kwamba angenifanya kuwa kusanyiko la mataifa na angenipa nchi hii kwa uzao wangu kama milki ya milele".

Tazama

Mungu alitumia neno hili "tazama" hapa kumuamsha Yakobo kuvuta nadhari kwa kile alichokuwa akitaka kumwambia.

nitakupa uzao mwingi, na kukuzidisha

Msemo "kukuzidishia" unaelezea jinsi ambavyo Mungu angemfanya Yakobo "kupata uzao". "Nitakupatia uzao mwingi sana"

Nitakufanya kuwa kusanyiko la mataifa

Hapa "nitakufanya" ina maana ya Yakobo, lakini ina maana ya uzao wa Yakobo. "Nitafanya vizazi vyako kuwa mataifa mengi"

milki ya milele

"milki ya kudumu"

Genesis 48:5

sasa

Hii haimaanishi "katika kipindi hiki" lakini inatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.

Efrahimu na Manase watakuwa wangu

Efrahimu na Manase kila mmoja atapokea sehemu ya nchi kama ndugu zake Yusufu.

watahesabiwa katika majina ya ndugu zao katika urithi wao

Maana zinawezekana kuwa 1) watoto wale wengine wa Yusufu wangerithi nchi kama sehemu ya makabila ya Efrahimu na Manase au 2) Yusufu atatengewa nchi na Efraimu na Manase na watoto wengine wa Yusufu watarithi nchi hiyo. "na kwa urithi wao, utawaorodhesha chini ya majina ya ndugu zao"

Efrathi

Hili ni jina lingine la mji wa Bethlehemu.

ndio, Bethlehemu

Mwandishi huyu anatoa taarifa ya nyuma.

Genesis 48:8

Ni nani hawa?

"Hawa ni watoto wa nani?"

niwabariki

Baba huwa anatamka baraka rasmi juu ya watoto au wajukuu wake.

Basi macho ya Israeli ... hakuweza kuona

Neno "Basi" linatumika hapa kuweka alama ya badiliko kutoka kwenye simulizi kwenda kwa taarifa ya nyuma kuhusu Israeli.

akawabusu

"Israeli aliwabusu"

Genesis 48:11

kuuona uso wako tena

Hapa "uso" ina maana ya mtu mzima. "Kukuona mara nyingine"

katikati ya magoti ya Israeli

Yusufu alipowaweka wanawe juu ya mapaja ya Israeli au magotini ilikuwa ishara ya kwamba Israeli alikuwa akiwachukua. Hii iliwapa watoto hawa urithi maalumu kutoka kwa Yakobo.

kisha akainama na uso wake juu ya nchi

Yusufu aliinama chini kuonyesha heshima kwa baba yake.

Manase katika mkono wake wa kulia kuelekea mkono wa kulia wa Israeli

Yusufu anawaweka wavulana ili kwamba Israeli aweze kuweka mkono wake wa kuume juu ya Manase. Manase alikuwa ndugu mkubwa na mkono wa kulia ilikuwa ishara ya kwamba angepokea baraka kubwa.

Genesis 48:14

mkono wake wa kulia na kuuweka juu ya kichwa cha Efrahimu

Kuweka mkono wa kulia juu ya kichwa cha Efraimu ilikuwa ishara ya kwamba angepokea baraka kubwa.

Israeli akambariki Yusufu

Hapa "Yusufu" pia ina maana ya Efraimu na Manase. Kwa kuwa Yusufu ni baba, ni yeye pekee anayetajwa hapa.

Mungu ambaye mbele zake baba zangu Ibrahimu na Isaka walitembea

Kumtumikia Mungu inazungumziwa kana kwamba ilikuwa kutembea mbele za Mungu. "Mungu ambaye babu yangu Abrahamu na baba yangu Isaka alimtumikia"

aliyenitunza

Mungu alimtunza Israeli kama vile mfugaji anavyotunza kondoo wake. "ambaye alinitunza kama mfugaji atunzavyo wanyama wake"

malaika

Maana zinawezekana kuwa 1) hii ina maana ya malaika ambaye Mungu alimtuma kumlinda Yakobo au 2) hii ina maana ya Mungu aliyemtokea kama malaika kumlinda Yakobo.

aliyenilinda

"aliniokoa"

Jina langu na litajwe kwao, na majina ya baba zangu Abrahamu na Isaka

Hapa "jina" lina maana ya mtu mzima. Msemo "jina langu na litajwe kwao" ni lahaja ambayo ina maana ya kwamba mtu anakumbukwa kwa sababu ya mtu mwingine. Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "Watu wamkumbuke Abrahamu, Isaka, na mimi kwa sababu ya Efraimu na Manase"

Na wawe makutano ya watu juu ya nchi

Hapa "wawe" ina maana ya Efraimu na Manase, lakini ina maana ya uzao wao. "Na wawe na uzao mwingi ambao utaishi ulimwenguni kote"

Genesis 48:17

ameweka mkono wake wa kulia juu ya kichwa

Mkono wa kulia ulikuwa ishara ya baraka kubwa ambayo mwana mkubwa alitakiwa kupokea.

Genesis 48:19

Yeye naye atakuwa watu, naye pia atakuwa mkuu

Hapa "yeye" ina maana ya Manase, lakini inahusu uzao wake. "Mwana wako mkubwa atakuwa na uzao mwingi, nao watakuja kuwa taifa kubwa"

siku hiyo kwa maneno haya

Hapa "maneno" ina maana ya kile kilichosemwa. "siku hiyo, akisema"

Watu wa Israeli watatamka baraka kwa majina yenu wakisema

"Watu wa Israeli watazungumza majina yenu pale wanapowabariki wengine"

kwa majina yenu wakisema, Mungu na akufanye kama Efrahimu na kama Manase

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Inaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "kwa majina yenu. Watamuuliza Mungu kuwafanya wengine kama Efraimu na kama Manase"

kama Efrahimu na kama Manase

Israeli kusema jina la Efraimu kwanza ni njia nyingine anaonyesha ya kwamba Efraimu atakuwa mkubwa kuliko Manase.

Israeli akamweka Efrahimu mbele ya Manase

Kumpatia Efraimu baraka kubwa na kumfanya awe wa muhimu kuliko Manase inazungumziwa kana kwamba Israeli amemuweka kihalisia wa mwili Efraimu mbele ya Manase.

Genesis 48:21

atakuwa nanyi ... atawarudisha ... baba zenu

Hapa "nanyi" na "zenu" ni wingi na ina maana ya watu wote wa Israeli.

atakuwa nanyi

Hii ni lahaja yenye maana ya Mungu atasaidia na kubariki watu wa Israeli. "Mungu atakusaidia" au "Mungu atakubariki"

atawarudisha

Hapa "atawarudisha" inaweza kutafsiriwa kama "kuchukua"

nchi ya baba zenu

"nchi ya mababu zenu"

Kwako wewe, kwa kuwa uko juu ya ndugu zako, ninakupa mtelemko wa mlima

Maana zinawezekana kuwa 1) Yusufu kuwa na heshima na mamlaka zaidi kuliko ndugu zake inazungumziwa kana kwamba alikuwa juu yao kiuhalisia wa kimwili. "Kwako, ambaye ni mkubwa kuliko ndugu zako, ninakupa mteremko wa mlima" au 2) Yakobo ana maanisha anatoa nchi zaidi kwa Yusufu kuliko anavyotoa kwa ndugu wa Yusufu. "Kwako, ninakupa kilima kimoja zaidi ya nayowapatia ndugu zako. Ninakupatia mteremko wa mlima"

Kwako wewe

Hapa "wewe" ni umoja na ina maana ya Yusufu.

mteremko wa mlima niliouchukuwa kutoka kwa Waamori kwa upanga wangu na upinde wangu

Hapa "upanga" na "upinde" ina maana ya kupigana vitani. "sehemu ya nchi niliyopigania na kuchukua kutoka kwa Waamori"

Genesis 49

Genesis 49:1

Maelezo ya Jumla:

Hii inaanza baraka za mwisho za Yakobo kwa wanawe. Hii inaendelea hadi 49:27. Baraka za Yakobo zinaandikwa kwa namna ya shairi.

Kusanyikeni ninyi wenyewe na msikilize, enyi wana wa Yakobo. Msikilizeni Israeli, baba yenu

Sentensi mbili zinasema jambo moja kuweka msisitizo. "Njooni na msikilize kwa makini baba yenu"

wana wa Yakobo. Msikilizeni Israeli, baba yenu.

Yakobo anajitambua katika lugha ya mtu wa utatu. Inaweza kusemwa katika lugha ya mtu wa kwanza. "wanangu. Nisikilizeni, baba yenu"

Genesis 49:3

mzaliwa wangu wa kwanza, nguvu zangu, na mwanzo wa uwezo wangu

Misemo ya "mzaliwa wangu wa kwanza, nguvu zangu" na "mwanzo wa uwezo wangu" zina maana moja. Maneno "uwezo" na "nguvu" yana maana ya uwezo wa Yakobo kuzaa watoto. Maneno "mzaliwa wa kwanza" na "mwanzo" ina maana ya kwamba Rubeni ni mwanawe wa kwanza. "mwanangu wa kwanza nilipokuwa mwanamume"

aliyesalia katika heshima na nguvu

Hii inaweza kuwekwa kama sentensi mpya. "Wewe ni wa kwanza kwa heshima na nguvu" au "Unawapita wengine wote kwa heshima na nguvu"

Asiyezuilika kama maji yarukayo

Yakobo anamlinganisha Rubeni na maji yenye mkondo mwenye nguvu kusisitiza ya kwamba hawezi kujizuia hasirayake na hayupo imara.

hautakuwa na umaharufu

"hautakuwa wa kwanza miongoni mwa ndugu zako"

kwa sababu ulikwenda juu ya kitanda cha baba yako. Hata ukakitia unajisi; ulipanda juu ya kitanda changu

Hapa "kitanda" na "juu ya kitanda changu" ina maana ya suria wa Yakobo, Bilha. Yakobo ana maanisha pale ambapo Rubeni alilala na Bilha. "kwa sababu ulipanda kitandani mwangu na kulala na Bilha suria wangu. Umeniaibisha"

ulikwenda juu ya kitanda cha baba yako ... ulipanda juu ya kitanda changu

Kaluli zote mbili zina maana moja.

Genesis 49:5

Simoni na Lawi ni ndugu

Hii haimaanishi tu ya kwamba wao ni ndugu kwa kuzaliwa. yakobo anasisitiza ya kwamba walishirikiana pamoja kuwaua watu wa Shekemu.

Panga zao ni silaha za vurugu

"Wanatumia panga zao kudhuru na kuua watu"

Ee nafsi yangu ... moyo wangu

Yakobo anatumia maneno "nafsi" na "moyo" kujitambulisha na kusema ya kwamba watu wengine, na labda Mungu pia, wanamheshimu sana ya kwamba hatamani kujiunga na wale wanaopanga kufanya uovu.

usiingie barazani pao; usiingie katika mikutano yao

Misemo hii miwili ina maana moja. Yakobo anaunganisha kuweka msisitizo ya kwamba hataki kushirikiana katika mipango yao miovu. "hakika sitajiunga nao kufanya mipango yoyote"

kuwakata visigino ng'ombe.

Hii ina maana ya Simoni na Lawi kulemaza ng'ombe kwa starehe tu.

kuwakata visigino

Hii ina maana ya kukata visigino vya miguu ya wanyama ili isiweze kutembea.

Genesis 49:7

Hasira yao na ilaaniwe, kwani ilikuwa kali - na ukali wao, kwani ulikuwa ni katili

Mungu kumlaani Simoni na Lawi inazungumziwa kana kwamba Mungu alikuwa akilaani hasira na ukali wao. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Bwana anasema, 'Nitawalaani kwa sababu ya hasira yao kali na ukali wao mkatili" au "Mimi, Bwana, nitawalaani kwa sababu ya hasira ya kali na ukali wao mkatili"

Hasira yao na ilaaniwe

Katika unabii, nabii mara nyingi huzungumza maneno ya Mungu kana kwamba Mungu mwenyenwe alikuwa akizungumza. Hii inasisitiza ukaribu ulivyo kati ya nabii na Mungu.

na ukali wao, kwani ulikuwa ni katili

Neno "nitalaani" linaeleweka. "nami nitalaani ukali wao, maana ulikuwa katili"

Nitawagawa katika Yakobo na kuwatawanya katika Israeli

Neno "Nitawagawa" lina maana ya Mungu. Neno "kuwatawanya" lina maana ya Simoni na Lawi lakini ni lugha nyingine yenye maana ya uzao wao. Maneno "Yakobo" na "Israeli" ni lugha nyingine yenye maana ya watu wote wa Israeli. "Nitawagawanya uzao wao na kuwasambaza miongoni mwa watu wote wa Israeli"

Genesis 49:8

ndugu zako watakusifu ... Wana wa baba yako watainama mbele zako

Kauli hizi mbili zina maana moja.

watakusifu. Mkono wako

Sentensi ya pili inaeleza sababu ya sentensi ya kwanza. Neno "kwa" au "kwa sababu" linaweza kuongezwa kuweka hii wazi. "nitakusifu wewe. Kwa mkono wako" au "nitakusifu kwa sababu mkono wako"

Mkono wako utakuwa shingoni mwa adui zako

Hii ni njia ya kusema. "Utawashinda adui zako"

watainama

Hii ina maana kuinama kwa unyenyekevu kuonyesha heshima na taadhima kwa mtu.

Genesis 49:9

Yuda ni mwana simba

Yakobo anamzungumzia Yuda kana kwamba alikuwa mtoto wa simba. Yakobo anasisitiza nguvu ya Yuda. "Yuda ni kama mwana wa simba"

Mwanangu, umetoka katika mawindo yako

"Wewe, mwanangu, umerudi kutoka kula windo lako"

kama simba jike

Yakobo anamlinganisha Yuda na simba jike. Simba jike ni mwindaji na mlinzi wa msingi wa watoto wake.

Je nani atakayejaribu kumwamsha?

Yakobo anatumia swali kusisitiza jinsi Yuda anavyotisha watu wengine. "Hakuna atakaye kumuamsha"

Genesis 49:10

Fimbo haitaondoka katika Yuda, wala fimbo ya utawala kutoka katika miguu yake

"Fimbo" na "fimbo ya utawala" ni miti iliyopambwa ambayo wafalme hubeba. Hapa ni lugha nyingine yenye maana ya nguvu ya utawala. Na "Yuda" ina maana ya uzao wake. "Nguvu ya kutawala daima itakuwa ndani ya uzao wa Yuda"

hata atakapo kuja Shilo. Mataifa yatamtii

Maana zawezekana kuwa 1) "Shilo" ina maana "shukrani". "hadi pale mataifa yatamtii na kuleta shukrani kwake" au 2) "Shilo" ina maana ya mji wa Shilo. "hadi pale mtawala atakuja Shilo. Kisha mataifa yatamtii." Watu wengi huchukulia hili kama unabii kuhusu Mesia ambaye ni uzao wa Mflame Daudi. Daudi ni uzao wa Yuda.

Mataifa yatamtii

Hapa "mataifa" ina maana ya watu. "Watu wa mataifa watamtii"

Genesis 49:11

Kumfunga punda wake ... katika mzabibu mzuri

Kauli zote mbili zina maana moja. Inasemekana ya kwamba mizabibu imejaa zabibu ambayo bwana hajali kama punda inavila baadhi yao.

wake ... amefua

Maana za muonakano wa "wake" au "amefua" ni 1) ina maana ya uzao wa Yuda. "wake ... wame" au 2) ina maana ya mtawala katika 49:10, ambayo inaweza kumaanisha Mesia.

amefua ... katika damu ya vichala vya mzabibu

Kauli zote mbili zina maana moja. Inasemekana ya kwamba kuna zabibu nyingi sana hadi wanaweza kufua nguo zao kwa maji yake.

amefua

Mara nyingi katika unabii matukio yatakoyotokea hapo baadae yanaelezwa kama jambo lililokwisha tokea zamani. Hii inasisitiza ya kwamba tukio hili hakika litatokea. "watafua" au "atafua"

damu ya vichala vya mzabibu

HIi inazungumzia kuhusu maji ya zabibu kana kwamba yalikuwa damu. Hii inasisitiza jinsi gani maji yalikuwa mekundu.

Macho yake yatakuwa meusi kama mvinyo

Hii ina maana ya rangi ya macho ya mtu kulinganisha na rangi ya mvinyo mwekundu. Maana zaweza kuwa 1) macho meusi ina maana macho yenye afya au 2) macho ya watu yatakuwa mekundu kutokana na kunywa mvinyo mwingi

meno yake meupe kama maziwa

Hii inalinganisha rangi ya meno ya watu kwa weupe wa rangi ya maziwa. Hii inasemekana ya kwamba kutakuwa na ng'ombe wengi wenye afya na kuwa na maziwa mengi ya kunywa.

Genesis 49:13

Zabuloni atakaa

Hii ina maana ya uzao wa Zabuloni.

Atakuwa bandari

Hapa "atakuwa" ina maana ya miji ya baharini ambayo watu wa Zabuloni wataishi au kujenga. Miji hii itatoa hifadhi kwa meli.

bandari

sehemu ya bahari ambayo ipo karibu na nchi na ipo salama kwa ajili ya meli.

Genesis 49:14

Isakari ni punda mwenye nguvu

Yakobo anazungumzia kuhusu Isakari na uzao wake kana kwamba walikuwa punda. Hii inasisitiza ya kwamba watafanya kazi kwa bidii. "Uzao wa Isakari utakuwa kama punda mwenye nguvu"

Isakari ni

Mara nyingi katika unabii matukio ambayo yatatokea baadae inaelezwa kama kitu ambacho tayari kinaendelea. Hii inasisitiza ya kwamba tukio litatokea hakika. Inaweza kuwekwa kwa lugha ya baade. "Isakari atakuwa" au "Uzao wa Isakari utakuwa"

Isakari ... Anaona ... Atainamisha

Hapa "Isakari" ni lugha nyingine yenye maana ya uzao wake. "Uzao wa Isakari ... Wanaona .. Wataona"

ajilazaye kati ya kondoo

Maana zaweza kuwa 1) "ajilazaye chini katikati ya kundi walizokuwa wakibeba" au 2) "ajilazaye chini katikati ya zizi la kondoo".Kwa namna yoyote ile, Yakobo anazungumzia kuhusu uzao wa Isakari kana kwamba walikuwa punda ambao wamefanya kazi kwa bidii na wamejilaza chini kupumzika.

mahali pazuri pa kupumzikia na nchi ya kupendeza

"sehemu ya kupumzikia ambayo ni nzuri na kwamba nchi inapendeza"

Atainamisha bega lake kwa mzigo

Msemo huu "Atainamisha bega lake kwa mzigo" ni njia ya kusema "fanya kazi kwa bidii kubeba mzigo"

kuwa mtumishi wake kwa kazi ile

"watafanya kazi kwa wengine kama watumwa"

Genesis 49:16

Dani atawaamua watu wake

Hapa "Dani" ina maana ya uzao wake. "Uzao wa Dani utawaamua watu wake"

watu wake

Maana zinazowezekana za "watu wake" ni 1) "watu wa Dani" au 2) "watu wa Israeli"

Dani atakuwa nyoka kando ya njia

Yakobo anazungumza kuhusu Dani na uzao wake kana kwamba walikuwa nyoka. Ingawa nyoka ni mdogo, inaweza kumshusha aongozaye farasi chini ya farasi wake. Kwa hiyo Dani, ingawa kabila dogo, ni la kutisha sana kwa adui zake. "Uzao wa Dani utakuwa kama nyoka kando ya barabara"

Ninaungoja wokovu wako, Yahwe.

Nomino inayojitegemea "wokovu" inaweza kutafsiriwa kama "kuokoa". "Ninakusubiri, Yahwe, kunikoa"

Ninaungoja

Neno "Ninaungoja" ina maana ya Yakobo.

Genesis 49:19

Gadi ... Asheri ... Naftali

Hawa ina maana ya vizazi vya kila mwanamume.

katika visigino vyao

Hapa "visigino" ina maana ya wavamizi ambao wanatoroka kutoka kwa uzao wa Gadi.

Vyakula vitakuwa vingi

Hapa "vingi" ni njia ya kusema "vitamu"

Naftali ni dubu jike asiyefungwa

Yakobo anazungumzia kuhuus uzao wa Naftali kana kwamba walikuwa paa wa kike ambaye yupo huru kukimbia. Hii inaweza kusisitiza ya kwamba watakuwa wajumbe wepesi. "Uzao wa Naftali utakuwa kama paa aliyeachiwa huru"

atakuwa na watoto wa dubu walio wazuri

"mtoto wa paa". Maana kwa lugha ya Kihebrania haipo wazi. Baadhi ya tafsiri hutafsiri kama "ana maneno mazuri" au "kuzungumza mambo mazuri"

Genesis 49:22

Yusufu ni tawi lizaalo

Hapa "Yusufu" ni lugha nyingine yenye maana ya uzao wake. Yakobo anazungumzia uzao kana kwamba walikuwa shina la mti lizaalo matunda mengi. Hii inasisitiza ya kwamba wataongezeka sana kwa idadi.

tawi

shina kuu la mti

ambaye matawi yake yako juu wa ukuta

Shina ambalo litakuwa na kusambaajuu ya ukuta inazungumziwa kana kwamba ilikuwa inapanda.

Genesis 49:24

Maelezo ya Jumla:

Yakobo anaendelea kumbariki Yusufu na uzao wake.

upinde wake utakuwa imara

Mtu anayeshikilia upinde kwa umakini inazungumziwa kana kwamba uoinde mwenyewe utakuwa imara. Inasemekana anaushikilia kwa ustadi anapopima kwa adui wake. "ataushika upinde wake kwa uimara anapolenga adui wake"

upinde wake ... mikono yake

Hapa "wake" ina maana ya Yakobo anayesimama badala ya uzao wake. "upinde wake .. mikono yake"

mikono yake itakuwa hodari

Hapa "mikono" ina maana ya mikono ya mtu anaposhikilia upinde wake kwa makini. "mikono yake utabaki imara anapolenga upinde wake"

mikono ya Mwenye nguvu

"mikono" inaelezea nguvu ya Yahwe. "nguvu ya Mwenye Nguvu"

kwa ajili ya jina la Mchungaji

Hapa "jina" lina maana ya mtu mzima. "kwa sababu ya Mchungaji"

Mchungaji

Yakobo anamzungumzia Yahwe kana kwamba alikuwa "mchungaji". Hii inasisitiza ya kwamba Yahwe anawaongoza na kuwalinda watu wake.

Mwamba

Yakobo anazungumzia kuhusu Yahwe kana kwamba alikuwa "Mwamba" ambao watu wanaweza kuupanda kutafuta usalama kutoka kwa maadui. Hii inasisitiza ya kwamba Yahwe hulinda watu wake.

Genesis 49:25

Maelezo ya Jumla:

Yakobo anaendelea kumbariki Yusufu na uzao wake.

atakusaidia ... atakubariki

Hapa "atakusaidia" ina maana ya Yusufu inayomaanisha uzao wake. "saidia uzao wako ... wabariki"

baraka za mbinguni juu

Hapa "mbinguni juu" ina maana ya mvua ambayo husaidia mazao kuota.

baraka za vilindi vilivyo chini

Hapa "chini" ina maana ya maji chini ya ardhi ambayo hutosheleza mito na visima.

baraka za maziwa na tumbo

Hapa "maziwa na tumbo" ina maana ya uwezo wa mama kupata watoto na kuwanyonyesha maziwa.

Genesis 49:26

Maelezo ya Jumla

Yakobo anaendelea kumbariki Yusufu na uzao wake.

milima ya zamani

Maana ya lugha asili haipo wazi. Baadhi ya tafsiri za Biblia zina "mababu zangu" badala ya "milima ya zamani"

Na viwe katika kichwa cha Yusufu

Hapa "viwe" ina maana ya baraka za baba yake.

juu ya taji ya kifalme kichwani pa ndugu zake

Yakobo anatamani kwa baraka hizi kupitishwa hata kwa wale wazawa muhimu. "juu ya kichwa cha mzawa muhimu wa Yusufu"

mwana wa mfalme kwa ndugu zake

"mtu muhimu wa ndugu zake"

Genesis 49:27

Benjamini ni mbwamwitu mwenye njaa

Hapa "Benyamini" ni lugha nyingine ya uzao. Yakobo anazungumzia juu ya uzao wa Benyamini kana kwamba ulikuwa mbwa mwitu wenye njaa. Hii inasisitiza ya kwamba watakuwa wapiganaji hodari. "Uzao wa Benyamini watakuwa kama mbwa mwitu"

Genesis 49:28

Haya ni makabila kumi na mbili ya Israeli

"Haya" ina maana ya wana wa Yakobo waliotajwa katika 49:1-27. Kila mwana alikuwa kiongozi wa kabila lake mwenyewe.

alipowabariki

Hapa neno "alipowabariki" lina maana ya kuongelea baraka rasmi.

kila mmoja kwa baraka iliyomstahili

"Akawapa kila mtoto baraka inayomstahili"

akawaelekeza

"akawaamuru"

Ninakaribia kwenda kwa watu wangu

Hii ni njia ya upole ya kusema ya kwamba amekaribia kufa. "Nimekaribia kufa"

kwenda kwa watu wangu

Yakobo ana maanisha pale ambapo nafsi yake utakwenda atakapokufa. Anategemea kuwaunga Abrahamu na Isaka katika maisha ya baadae.

Efroni Mhiti

Hili ni jina la mwanamume. "Mhiti" ina maana ya "uzao wa Hethi".

Makpela

Makpela lilikuwa jina la eneo au mahali.

Mamre

Hili lilikuwa jina lingine la mji wa Hebroni. Inawezekana lilitajwa baada ya Mamre, rafiki wa Abrahamu aliyeishi kule.

Genesis 49:31

Maelezo ya Jumla:

Yakobo anaendelea kuzungumza na wanawe.

lililomo lilinunuliwa

Ununuzi unaweza kuwekwa wazi. "ndani mwake ulinunuliwa na Abrahamu"

kutoka kwa watu wa Hethi

"kutoka kwa Wahiti"

alipomaliza maagizo hayo kwa wanawe

"alimaliza kuwaagiza wanawe" au "alimaliza kuwaamuru wanawe"

akaiweka miguu yake kitandani

Yakobo alikuwa amekaa juu ya kitanda. Sasa, Yakobo anageuka na kuweka miguu yake kitandani ili aweze kulala chini.

akavuta pumzi ya mwisho

Hii ni njia ya upole ya kusema mtu amekufa.

akawaendea watu wake

Baada ya Yakobo kufa, nafsi yake ilikwenda sehemu ile ile kama ndugu zake waliokufa kabla yake.

Genesis 50

Genesis 50:1

akauangukia uso wa baba yake

Msemo "akauangukia" ni lahaja ya kuzidiwa. "hadi akaanguka juu ya baba yake kwa majonzi"

watumishi wake matabibu

"watumishi wake ambao waliangalia maiti"

kumtia dawa babaye

"kumtia dawa" ni njia maalumu ya kuhifadhi maiti kabla haijazikwa. "kuandaa mwili wa baba yake kabla ya mazishi"

Wakatimiza siku arobaini

"Wakatimiza siku 40"

siku sabini

"siku 70"

Genesis 50:4

Siku za maombolezo

"siku za kumuomboleza" au "siku za kumlilia"

Yusufu akaongea na watumishi wa baraza la kifalme

Hapa "baraza la kifalme" ina maana ya maafisa ambao huunda baraza la kifalme la Farao. "Yusufu alizungumza na maafisa wa Farao"

Ikiwa nimepata kibali machoni penu

Msemo "machoni penu" ni lugha nyingine yenye maana ya fikra na mawazo ya Yakobo. "Iwapo nimepata kibali kwako" au "kama umefurahishwa na mimi"

nimepata kibali

Hii ni lahaja yenye maana ya kwamba mtu amekubalika na mtu mwingine.

tafadhali ongeeni na Farao, kusema, 5'Baba yangu aliniapisha, kusema, "Tazama, ninakaribia kufa. Unizike katika kaburi nililolichimba kwa ajili yangu mwenyewe katika nchi ya Kanaani. Ndipo utakaponizika." Basi sasa niruhusu niende nimzike baba yangu, na kisha nitarudi."

Hii ina madaraja mawili ya nukuu na madaraja matatu ya nukuu. Hizi zinaweza kuwekwa kama nukuu zisizo moja kwa moja. "tafadhali mwambie Farao ya kwamba baba yangu alinifanya niape ya kuwa baada ya kufa kwake nitamzika katika kaburi ambalo alilichimba kwa ajili yake katika nchi ya Kaanani. Tafadhali muombe Farao aniruhusu niende kumzika baba yangu, na kisha nitarudi.

Tazama, ninakaribia kufa

"Tazama, ninakufa"

niruhusu niende juu

Ilikuwa kawaida kutumia msemo "kwenda juu" pale izungumzwapo safari ya kutoka Misri kwenda Kaanani.

Farao akajibu

Inasemekana ya kwamba wajumbe wa baraza walizungumza na Farao, na sasa Farao anamjibu Yusufu.

kama alivyokuwapisha

"kama ulivyoapa kwake"

Genesis 50:7

Yusufu akaenda juu

Ilikuwa kawaida kutumia msemo "kwenda juu" inapozungumziwa safari ya kutoka Misri kwenda Kaanani.

Maofisa wote ... washauri ... maofisa waandamizi

viongozi wote muhimu wa Farao walihudhuria tukio la mazishi.

washauri

Huyu mtu alikuwa mshauri wa kifalme.

washauri wa nyumba yake

Hapa "nyumba" ina maana ya baraza la kifalme la Farao.

nchi ya Misri, pamoja na nyumba yote ya Yusufu na ndugu zake, na nyumba yote ya baba yake

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. "nchi ya Misri. Nyumba ya Yusufu, ndugu zake, na nyumba ya baba yake walikwenda naye"

nyumba ya Yusufu ... nyumba ya baba yake

Hapa "nyumba" ina maana ya familia zao.

Vibandawazi

Hapa ina maana ya wanamume wanaoendesha ndani ya vibandawazi.

Lilikuwa kundi kubwa sana la watu

"ulikuwa mkusanyiko mkubwa sana"

Genesis 50:10

Hata walipokuja

Neno "walipokuja" lina maana ya washiriki katika tukio la mazishi.

sakafu ya Atadi

Maana zaweza kuwa 1) neno la "Atadi" lina maana ya "mwiba" na lina maana ya sehemu ambapo kuna idadi kubwa ya miiba inayoota, au 2) inaweza kuwa jina la mtu anayemiliki sakafu ya kupigia.

wakaomboleza kwa majonzi ya huzuni kubwa

"walikuwana huzuni kubwa na walilia sana"

ya siku saba

"ya siku 7"

katika sakafu ya Atadi

"katika sakafu ya kupigia ya Atadi"

Hili ni tukio la kuhuzunisha sana kwa Wamisri

"maombolezo ya Wamisri ni mkubwa sana"

Abeli Mizraimu

"Jina la Abeli Mizraimu lina maana ya "maombolezo ya Misri"

Genesis 50:12

wanawe

"Kwa hiyo wana wa Yakobo"

kama alivyokuwa amewaagiza

"kama alivyokuwa amewaagiza"

Wanawe wakambeba

"Wanawe waliuchukua mwili wake"

Makpela

Makpela ni jina la jina la eneo au sehemu.

Mamre

Hili lilikuwa jina jingine la mji wa Hebroni. Inawezekana lilikuwa jina baada ya Mamre, rafiki wa Abrahamu aliyeishi kule.

Efroni Mhiti

Hili ni jina la mwanamume. "Mhiti" ina maana ya "uzao wa Hethi"

Yusufu akarudi Misri

"Yusufu alirudi Misri"

wote waliokuwa wamemsindikiza

"wale wote waliokuja pamoja nami"

Genesis 50:15

Itakuwaje ikiwa Yusufu atatukasirikia

Hapa hasira inazungumziwa kana kwamba ilikuwa kitu cha kimwili ambacho Yusufu alikishika kwa mkono wake. "Je iwapo Yusufu atakuwa bado na hasira na sisi"

akataka kutulipa kikamilifu kwa ajili ya uovu tuliomtenda

Kulipiza mwenyewe dhidi ya mtu mwingine aliyemdhuru inazungumziwa kana kwamba mtu alikuwa akilipa mtu mwingine kile walichodai. "anataka kulipiza kwa uovu tuliofanya kwake"

Baba yako alitoa maelekezo kabla hajafa, kusema, 'Mwambieni hivi Yusufu, "Tafadhali samehe makosa ya ndugu zako na dhambi yao uovu waliokutenda."

Hii ina madaraja mawili ya nukuu na madaraja matatu ya nukuu. Zinaweza kuwekwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Baba yako alituagiza kabla ya kufa tukuambie ya kwamba utusamehe kwa uovu tuliokufanyia kwako"

Baba yako alitoa maelekezo kabla hajafa, kusema

Yakobo alikuwa baba wa ndugu wote. Hapa wanasema "baba yako" kusisitiza ya kwamba Yusufu anahitaji kuvuta nadhari kwa kile baba yake alichosema. "Kabla baba yetu hajafa alisema"

na dhambi yao uovu waliokutenda

"kwa mambo maovu waliyokufanyia kwako"

Basi

Hii haimaanishi "katika kipindi hiki" lakini inatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu linalofuata.

Basi wasamehe watumishi wa Mungu wa baba yako

Ndugu wanajitambulisha kama "watumishi wa Mungu wa baba yako". Hii inaweza kuwekwa katika lugha ya mtu wa kwanza. "tafadhali tusamehe, watumishi wa Mungu wa baba yetu"

Yusufu akalia walipomwambia.

"Yusufu alilia aliposikia ujumbe huu"

Genesis 50:18

kuinamisha nyuso zao mbele zake

Walilala chini kifudifudi kuelekea ardhini. Hii ni ishara ya unyenyekevu na heshima kwa Yusufu.

Je mimi ni badala ya Mungu?

Yusufu anatumia swali kuwatia moyo ndugu zake. "Mimi sipo katika nafasi ya Mungu" au "Mimi sio Mungu"

mlikusudia kunidhuru

"mlikusudia kutenda uovu dhidi yangu"

Mungu alikusudia mema

"Mungu alikusudia kwa wema"

Hivyo basi msiogope

"Kwa hiyo msiniogope"

Nitawahudumia ninyi na watoto wenu wadogo

"Nitahakikisha nyie pamoja na watoto wenu mnapata chakula cha kutosha"

aliwatia moyo na kuongea na mioyo yao kwa upole.

"Aliwatia moyo kwa kuzungumza nao kwa upole"

Genesis 50:22

miaka mia moja na kumi

"miaka 110"

Efraimu hata kizazi cha tatu

"Watoto na wajukuu wa Efraimu"

Makiri

Hili ni jina la mjukuu wa Yusufu"

waliowekwa katika magoti ya Yusufu

Msemo huu una maana ya kwamba Yusufu alitwaa watoto hawa wa Makiri kama watoto wake. Hii ina maana wangekuwa na haki ya urithi maalumu kutoka kwa Yusufu.

Genesis 50:24

atawajilia

Katika 50:24 neno "atawajilia" lina maana ya ndugu wa Yusufu, lakini pia lina maana ya uzao wake.

kuwaongoza kutoka katika nchi hii na kuwapeleka katika nchi

Ilikuwa kawaida kutumia msemo wa "kupanda" kuzungumzia safari ya kutoka Misri kwenda Kaanani. "kuwaleta kutoka nchi hii na kuwapeleka katika nchi"

Wakampaka dawa

"kumpaka dawa" ni njia maalumu ya kuhifadhi maiti kabla haujazikwa.

akawekwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "walimweka"

katika jeneza

"ndani ya sanduku" au "katika kasha". Hili ni sanduku ambalo mtu aliyekufa kuwekwa ndani.

Exodus 1

Exodus 1:1

jamii

Hii inahusu watu wote wanao ishi katika nyumba pamoja, hususani familia kubwa yenye watumishi.

sabini

"70"

yusufu alikuwa Misri tayari

"Yusufu aliishi Misri kabla ya kaka zake"

Exodus 1:6

kaka zake wote

kaka zake wakubwa 10 na mdogo 1.

Walikuwa wamatunda

Uzao wa watoto kwa Waisraeli unasemekana kama vile mimea inayo zaa matunda.

nchi ili jazwa nao

Hii ya weza wekwa kwenye tensi tendaji. "Walijaza nchi"

pamoja nao

Neno "wao" la husu Waisraeli.

Exodus 1:8

akainuka juu ya Misri

Hapa "Misri" ya husu watu wa Misri.

Akasema kwa watu wake

"Mfalme akasema kwa watu wake"

watu wake

Hawa walikuwa watu waliyo ishi Misri, Wamisri.

na tufanye

Neno "sisi" lina jumuisha na kuhusu mfalme na watu wake, Wamisri.

Vita vikalipuka

Hapa vita vinatajwa kama mtu anaye weza kufanya matendo.

kuondoka nchini

"kuondoka Misri"

Exodus 1:11

mabwana wa kazi

"waendesha watumwa." Hawa walikuwa Wamisri ambao kazi yao ilikuwa kulazimisha Waisraeli kufanya kazi ngumu.

kuwa kandamiza kwa kazi ngumu

"kuwa lazimisha Waisraeli kufanya kazi ngumu ya Wamisri"

miji ya ghala

Hizi zilikuwa sehemu viongozi walipo weka chakula na vitu vingine muhimu kuviweka salama.

Exodus 1:13

kufanya ... kazi kwa juhudi

"kufanya ... fanya kazi kwa nguvu" au "kwa vikali fanya ... kazi"

walifanya maisha yao machungu

Maisha magumu ya Waisraeli yanazungumzwa kama vile yalikuwa chakula kichungu ambacho kili kuwa kigumu kula.

chokaa

Hii ilikuwa gundi ya maji au matope kati ya matofali au mawe yaliyo yashika pamoja yalipo kauka.

Kazi zao zote zilikuwa ngumu

"Wamisri waliwafanya wafanye kazi kwa nguvu sana" au "Wamisri waliwalimizimisha kufanya kazi kwa ngumu"

Exodus 1:15

mfalme wa Misri

Wafalme wa Misri aliitwa Farao.

wakunga

Hawalikuwa wanawake waliyo wasaidia mwanawake kuzaa mtoto.

Shifira ... Pua

Haya ni majina ya wanawake wa Kiebrania.

katika kiti cha kujifungulia

Wanawake waliketi kwenye ichi kiti walipo jifungua. Hivyo basi, ina hashiriwa na kujifungua.

Exodus 1:18

wakunga

Ona jinsi ulivyo tafsiri 1:15

Kwanini umefanya hivyo, na kuwaacha watoto kuishi?

Farao aliuliza hili swali kukemea wakunga kwa kuruhusu watoto kuishi.

Wanawake wa Kiebrania hawapo kama wanawake wa Kimisri

Wakungu walijibu kwa hekima kuridhisha hasira ya Farao.

Exodus 1:20

Nini Farao aliagiza watu wake kufanya kwa watoto wa kiume?

Farao aliagiza watu wake wote, "Lazima mtupe kila mtoto wa kiume anaye zaliwa kwenye mto."

Exodus 2

Exodus 2:1

Sasa

Neno hili linatumika hapa kuweka alama ya mapumziko katika matukio muhimu. Hapa mwandishi anaanza kusimulia sehemu mpya.

tatu

"3"

Exodus 2:3

kisafina cha manyasi

Hichi ni chombo kilicho tengenezwa kutokana nyasi inayo ota kando ya Mto wa Misri.

akakipaka sifa na lami

Unaeza elezea kuwa hii ilikuwa kwa ajili ya kuzuuia maji.

sifa

Hii ni gundi iliyo tengenezwa kwa petroli. Yaweza kutumika kuzuia maji.

lami

Hii ni gundi ya rangi kawia au nyeusi inayo weza kutengenezwa kwa utomvu wa mti au petroli. Hivyo basi "lami" itajumuisha sio tu "sifa" bali pia mimea yenye utomvu. Yaweza tumika kuzuia maji.

majani

Haya "majani" yalikuwa haina ya nyasi ndefu yaliyo ota sehemu nyevu na tambarare.

akasimama mbali

Hii ina maana ya kuwa alisimama umbali ambao hakuweza kuonekana, lakini kwa ukaribu ambao aliweza kuona sanduku.

Exodus 2:5

vijakazi

"watumishi"

Tazama

Neno "Tazama" la hashiria maelezo yanayo shangaza yafuatayo.

Exodus 2:7

akunyonyeshe

"kunyonyesha"

Exodus 2:9

akamleta

"mwanamke wa Kiebrania akamleta"

akawa mwana wake

"akawa mwana wa kupanga wa binti wa Farao"

Kwasababu nilimtoa kwenye maji

Watafsiri wanaweza kuongeza alama inayo sema "Jina Musa linaeleweka kama jina la Kiebrania linalo maanisha "kuvuta."

nilimtoa

"kumvuta"

Exodus 2:11

akampiga

"kumgonga"

Akatazama huko na huko

Haya maeneo tofauti yana maana moja ya "kila sehemu."

Exodus 2:13

Akatoka

"Musa akatoka"

Tazama

Neno "tazama" hapa la onyesha kwamba Musa alishangazwa kwa alicho kiona.

yeye aliye kuwa na makosa

Hii ilikuwa ni namna ya kusema "yeye alianza pambano"

nani aliye kufanya kiongozi na muamuzi juu yetu?

Mtu aliye tumia hili swali kumkemea Musa kwa kuingilia pambano.

Unataka kuniua kama ulivyo muua yule Mmisri?

Mwanaume huyu alitumia swali kwa kejeli.

Exodus 2:15

Sasa Farao alipo sikia kuhusu hili

Neno "sasa" linatumika hapa kuweka alama ya pumziko katika tukio. Hapa mwandishi anaanza kueleza sehemu mpya ya tukio.

Sasa kuhani wa Midiani alikuwa na mabinti saba

Neno "sasa" linatumika hapa kuweka alama ya pumziko katika tukio. Hapa mwandishi anaeleza watu wapya katika simulizi.

chota maji

Hii ina maana walichota maji kwenye kisima.

birika

chombo kirefu cha wazi, chemba, kinacho wanacho tumia wanyama kulia au kunywea.

kuwafukuza

"kuwakimbiza"

akawasaidia

"akawaokoa"

Exodus 2:18

Kwanini ulimuacha mwanaume?

Hili swali ni kemeo kwa mabinti kwa kutomkaribisha Musa nyumbani kwao kwa kadiri ya mapokezi ya utamaduni.

Exodus 2:21

Musa akakubali kukaa na huyo mwanaume

"Musa akakubali kuishi na Reueli"

Zipora

Huyu ni binti wa Reueli.

Gerishomu

Huyu ni mwana wa Musa

wakazi katika nchi ya kigeni

"wageni katika nchi ya kigeni"

Exodus 2:23

sononeka

Walifanya hivi kwasababu ya uzuni na mateso yao.

maombi yao yakaenda kwa Mungu

kilio chao Waisraeli kikaenda kinazungumziwa kama ni mtu na anaweza kwenda Mungu alipo.

Mungu akakumbuka agano lake

Hii ilikuwa namna ya kitamaduni yakusema Mungu aliwaza kuhusu alicho kiahidi.

Exodus 3

Exodus 3:1

malaika wa Yahweh

Huyu alikuwa Yahweh mwenyewe aliyekuwa anajitokeza kama malaika, na sio kama malaika Yahweh aliye mtuma.

Yahweh

Hili ni jina la Mungu alilo lirihidhisha kwa watu wake wa Agano la Kale.

Tazama

Neno "tazama" hapa linaonyesha kwamba Musa aliona kitu kilicho kuwa cha tofauti na alicho tegemea.

Exodus 3:4

kutengwa

"kilicho fanywa takatifu"

Mungu wa baba yako, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo

Hawa wanaume wote walimuabudu Mungu mmoja.

baba yako

Maana inayo wezekana ni 1) "babu yako" au 2) "baba yako." Kama ina maana babu yako," kisha basi maneno yafuatayo ya fafananua nani "baba yako" ina muhusu: ina muhusu Ibrahimu, Isaka, na Yakobo. Kama ina maana ya "baba yako," kisha basi ina muhusu baba yake Musa.

Exodus 3:7

wasimamizi

"waendesha watumwa." Hawa walikuwa wa Misri ambao kazi yao ilikuwa kuwalazimisha Waisraeli kufanya kazi.

nchi inayo tiririka kwa maziwa na asali

"nchi ambayo maziwa na asali yatiririka." Mungu akazungumza kwa habari ya nchi kuwa nzuri kwa ajili ya wanyama na mimea kama maziwa na asali kutoka kwa hao wanyama na mimea ilikuwa ya tiririka kwenye nchi.

tiririka kwa

"imejawa na" au "na utele wa"

maziwa

Kwa maana maziwa yanatoka kwa ng'ombe na mbuzi, hii yawakilisha chakula kinacho tokana na mifugo.

asali

Kwa maana asali yatokana na mau, hii ya wakilisha chakula cha mazao.

Exodus 3:9

kelele za watu Waisraeli zimekuja kwangu

Hapa neno "kelele" inazungumziwa kama ni watu wanao weza kusogea mwenyewe.

Exodus 3:11

Mimi ni nani, hadi niende kwa Farao ... Misri?

Musa anatumia hili swali kumuambia Mungu kwamba Musa sio kitu na hakuna atakaye msikiliza.

Exodus 3:13

Mungu akamwambia Musa, "MIMI NIKO AMBAYE NIKO."

Hili ndilo jibu la Mungu kwa swali la Musa kuhusu jina la Mungu.

MIMI NIKO AMBAYE NIKO

Maana inayo wezekana hapa ni 1) hii sentesi yote ni jina la Mungu au 2) Mungu hasemi jina lake lakini kitu kuhusu yeye. Kwa kusema hili, Mungu anafundisha kuwa yeye ni wa milele; aliishi na ataishi.

Exodus 3:16

Maelezo ya Jumla

Mungu anaendelea kuzungumza na Musa.

Mungu wa mababu zako, Mungu wa Ibrahimu, wa Isaka, na wa Yakobo

Ibrahimu, Isaka na Yakobo walikuwa ni mababu wa tatu wa Musa. Wote walimuabudu Mungu mmoja.

Hakika nimekutathimini

Neno "wewe" la husu watu wa Israeli.

nchi inayo tiririka maziwa na asali

Mungu aliongelea nchi kuwa nzuri kwa wanyama na mimea kana kwamba maziwa na asali kutoka kwa hao wanyama yalikuwa ya tiririka kwenye nchi.

tiririka

"iliyo jawa" au kwa utele wa"

maziwa

Kwa maana maziwa yanatoka kwa ng'ombe na mbuzi, hii ya wakilisha chakula kinacho tokana na mifugo.

asali

Kwa maana asali yanatoka kwenye mau, hii ya wakilisha chakula kinacho tokana na mazao.

Watakusikiliza wewe

Neno "wewe" la muhusu Musa.

Exodus 3:19

Maelezo ya Jumla

Mungu anaendelea kusema na Musa.

hadi mkono wake ulazimishwe

Hii yaweza andikwa katika tenzi tendaji. Neno "mkono" linasimama katika nafasi ya nguvu ya mwenye mkono. Maana inayo wezekana ni 1) "pale tu atakapoona hana nguvu ya kufanya kitu kingine chochote" 2) "pale tu nitakapo mlazimisha kuacha muende" au 3) "ata kama nitamlazimisha kuwaacha muende"

Nitanyoosha mkono wangu na kushambulia

Hapa "mkono" wa husu nguvu ya Mungu.

sitaenda mikono mitupu

Hapa neno "mikono mitupu" linatumika kueleza maana tofauti.

wanawake wowote wanao ishi nyumbani kwa jirani

"Misri yeyote anaye ishi nyumbani kwa jirani yake wa Kimisri"

Exodus 4

Exodus 4:1

kama wasipo amini

"kama Waisraeli wasipo amini"

Exodus 4:4

shika kwenye mkia

"nyanyua kwenye mkia" au "chukuwa kwenye mkia"

likawa gongo

"geuka kuwa gongo" au "badilika kuwa gongo"

Mungu wa mababu zao, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo

Ibrahimu, Isaka na Yakobo walikuwa ni mababu wa tatu wa Musa. Wote walimuabudu Mungu mmoja.

Exodus 4:6

tazama

Hili neno linatumika kuweka mshangao

nyeupe kama theluji

Neno "kama" hapa linatumika kulinganisha mkono wa Musa ulivyo onekana. Ukoma una sababisha ngozi kuonekana nyeupe.

Exodus 4:8

kuwa makini

"tambua" au "kubali"

Exodus 4:10

mnenaji hodari

"mnenaji mzuri"

mimi ni mtaratibu wa kuongea na mtaratibu wa ulimi

Haya maneno "mtaratibu wa kuongea" na "mtaratibu wa ulimi" yana maana moja. Musa alitumia kuwe mkazo kuwa sio msemaji mzuri.

mtaratibu wa ulimi

Hapa "ulimi" wa husu Musa na uwezo wake wa kuongea.

Nani aliye ufanya mdomo wa mwanadamu?

Yahweh anatumia swali kuweka mkazo kwamba yeye ni muumbaji anaye wezesha watu kuzungumza.

Nani anaye mfanya mtu bubu au kiziwi au kuona au kipofu?

Yahweh anatumia swali kuweka mkazo kwamba yeye ndiye anaye amua kama watu wataongea na kusikia, na kama wataona.

Siye mimi, Yahweh?

Yahweh anatumia swali kuweka mkazo kwamba yeye ndiye mwenye maamuzi haya.

nitakuwa na mdomo wako

Hapa "mdomo" wa husu Musa na uwezo wake wakuongea.

Exodus 4:14

ata kuwa na furaha moyoni mwake

Hapa "moyo" wa husu mawazo ya ndani na hisia.

eka maneno ya kusema modomoni mwake

Maneno hapa yanazungumzwa kama ni vitu vinavyo weza kuwekwa mdomoni mwa mtu. Hapa maneno yana maana ya ujumbe.

nitakuwa na mdomo wako

Neno "mdomo" hapa lina wakilisha uchaguzi wa maneno ya Musa.

mdomo wake

Neno "mdomo" hapa lina wakilisha uchaguzi wa maneno ya Aruni.

Ata kuwa na mdomo wako

Neno "mdomo" hapa lina wakilisha marudio ya yale Aruni aliyo ambiwa na Musa.

utakuwa kwake kama kwangu, Mungu

Neno "kama" hapa la maanisha Musa ata wakilisha mamlaka hayo kwa Aruni kama Mungu alivyo fanya kwa Musa.

Exodus 4:18

baba mkwe

Hii ya husu baba wa mke wa Musa.

Exodus 4:21

ata fanya moyo wake mgumu

Hapa "moyo" wa husu Farao. Tabia yake ya kiburi inazungmziwa kama moyo wake ni mgumu.

Israeli ni mwana wangu

Neno "Israeli" hapa lina wakilisha watu wote wa Israeli.

ni mwana wangu, mzaliwa wangu wa kwanza

Hapa watu wa Israeli wanazungumziwa kama wazaliwa wa kwanza anaye sababisha furaha na kiburi.

Nitaua mwanao hakika, mzaliwa wako wa kwanza

Neno "mwana" hapa la husu mwana halisi wa Farao

Exodus 4:24

Yahweh alikutana na Musa na akajaribu kumuua

Hii yaweza kuwa kwasababu Musa hakumtairi mwanae.

Zipora

Hili ni jina la mke wa Musa

kisu cha jiwe

Hichi kilikuwa kisu kliicho undwa kwa jiwe.

kwenye miguu yake

Ina wezekana kuwa neno "miguu" hapa limetumika kama namna ya heshima ya kutaja sehemu zake za siri za mwili.

wewe ni bwana arusi kwangu kwa damu

Maana ya umbo hili sio wazi. Yaweza kuwa ulikuwa msemo unao fahamika kwenye utamaduni wao.

Exodus 4:27

Yahweh akamwambia Aruni

Unaweza taka kuongeza neno linalo weza kuweka alama mwanzo wa sehemu mpya wa hadithi.

katika mlima wa Mungu

Huu waweza kuwa mlima wa Sinai, lakini ukurasa hauelezi maelezo haya.

alimtuma yeye kusema

Neno "yeye" lamuhusu Yahweh.

Exodus 4:29

katika macho ya watu

"mbele ya watu" au "katika uwepo wa watu"

aliwatathimini Waisraeli

"aliwaona Waisraeli" au "alijali kuhusu Waisraeli"

waliinamisha vichwa vyao

Maana zinazo wezakana ni 1) "aliinamisha vichwa vyao kwa mshangao" au 2) "aliinama chini kwa kuabudu"

Exodus 5

Exodus 5:1

Baada ya hivi vitu kutokea

Sio wazi muda gani ambao Musa na Aruni walisubiri mpaka walipo muuona Farao.

sherehe kwa ajili yangu

Hii ni sherehe ya kumuabudu Yahweh.

Yahweh ni nani?

Farao anatumia hili swali kuonyesha kuwa hamtambui Yahweh kama mungu halali.

Kwanini mimi ... ach Israeli iende?

Farao anatumia hili swali kuonyesha kwamba anatamanio la kumtii Yahweh au kuwaacha Waisraeli waende kumuabudu Mungu.

sikiliza sauti yako

Maneno "sauti yako" yana wakilisha Mungu aliyo ya sema.

Exodus 5:3

Mungu wa Waebrania

Hili ni neno linalo tumika kwa ajili ya Mungu wa Waisraeli au Yahweh.

au kwa upanga

Hapa "upanga" ya wakilisha vita au shambulizi la maadui.

kwanini unachukuwa watu kutoka kazini kwao?

Farao anatumia swali hili kuonyesha hasira yake kwa Musa na Aruni kuwatoa Waisraeli kwenye kazi yao.

Exodus 5:6

wasimamizi

"waendesha watumwa" Hawa walikuwa Wamisri ambao kazi yao ilikuwa kuwalazimisha Waisraeli kufanya kazi ngumu.

wewe haupaswi kutoa tena

Neno "wewe" katika hii mistari ni wingi na ya husu wasimamizi na mabwana.

Exodus 5:10

wasimamizi

"waendesha watumwa" Hawa walikuwa Wamisri ambao kazi yao ilikuwa kuwalazimisha Waisraeli kufanya kazi ngumu.

sitakupatia wewe mrija wowote tena .. pata mriji popote utakapo upata

Neno "wewe" katika hii mistari ni wingi na ya husu watu wa Israeli.

nyinyi wenyewe lazima muende

Hapa "wenyewe" la tilia mkazo kuwa Wamisri hawata wasaidia.

mzigo wa kazi zenu hazitapunguzwa

Hii yaweza andikwa katika mfumo endelevu.

Exodus 5:12

nchi yote ya Misri

Huu ni msisitizo wa kuonyesha juhudi la ziada

wasimamizi

"waendesha watumwa" Hawa walikuwa Wamisri ambao kazi yao ilikuwa kuwalazimisha Waisraeli kufanya kazi ngumu.

kapi

sehemu ya mmea ambayo inabaki baada ya mavunop

kwanini ujatengeneza matofali yote yanayo kupasa ... hapo awali?

Wasimamizi walitumia maswali kuonyesha wana hasira kwa upungufu wa matofali.

Exodus 5:15

wakalia

"wakalalamika"

bado wanatuambia 'tengeneza matofali!'

Hapa "wana" ya husu wasimamizi wa Kimisri.

Exodus 5:19

walipo ambiwa

Hii yaweza andikwa katika sentensi tendaji.

jumba

Hii ni nyumba kubwa sana mfalme anayo ishi.

mmetufanya chukizo

Wamisri wali wajibu Waisraeli kama walivyo kuwa wakijibu wanapo sikia harafu chafu.

wameweka upanga mkononi mwetu kutuua

Hapa "upanga" wawakilisha nafasi ya kuteketeza maadui.

Exodus 5:22

Bwana kwanini umesababisha matatizo kwa hawa watu?

Hili swali la onyesha jinisi alivyo kata tamaa kuwa Wamisri wana wa tendea vibaya Waisraeli kwa ukali zaidi sasa.

kwanini ulinituma mimi kwanza?

Hili swali la onyesha jinsi Musa alivyo kata tamaa kuwa Mungu alimtuma Misri.

ongea nae kwa jina lake

Neno "jina" hapa la wakilisha ujumbe wa Mungu.

Exodus 6

Exodus 6:1

mkono wangu hodari

Neno "mkono" hapa wa wakilisha matendo ya Mungu au kazi.

Exodus 6:2

Nilimtokea Ibrahimu, Isaka, na Yakobo

"Nilijionyesha kwa Ibrahimu, Isaka, na Yakobo"

sikujuliikana kwao

Hii yaweza andikwa katika sentensi tendeaji.

kilio

Hii ina maana ya kufanya sauti za uzuni kwasababu ya maumivu na mateso.

Exodus 6:6

sema kwa Waisraeli

Hii ni amri kutoka kwa Yahweh kwa Musa.

Exodus 6:8

muahidi

"apa" au "niliyo sema nita"

Exodus 6:10

Kama Waisraeli hawajanisikiliza mimi , kwa nini Farao anisikillize mimi, tangu mimi sio mzuri wakuzungumza?

Musa aliuliza hili swali akitumaini Mungu atabadilisha nia yake ya kumtumia Musa.

Exodus 6:14

vichwa wa nyumba za baba yao

Hapa "vivhwa" ya husu mababu wa hasili wa ukoo.

Hanoki ... Shauli

Haya ni majina ya wanaume.

Exodus 6:16

Gerishoni ... Merari

Haya ni majina ya wanaume.

Amramu ... Uzieli

Haya ni majina ya wanaume.

Exodus 6:20

Izhari ... Kora ... Zikri

Haya ni majina ya wanaume.

Uzieli .. Mishaeli ... Sithri

Haya ni majina ya wanaume.

Exodus 6:23

Nadabu ... Ithamari

Haya ni majina ya wanaume.

Fineazi

Haya ni majina ya wanaume.

Hawa walikuwa vichwa wa nyumba za baba yao

Neno "vichwa" ya wakilisha viongozi wa familia.

Exodus 6:26

kwa makundi ya wanaume wapiganaji

"kabila moja kwa wakati" au "kundi la familia moja baada ya lingine"

Exodus 6:28

Mimi sio mzuri ... kwanini Farao anisikilize mimi?

Musa anauliza hili swali akitumaini kubadilisha nia ya Mungu.

Exodus 7

Exodus 7:1

nimekufanya kama mungu

"nitamsabisha Farao akuchukulie kama mungu"

Exodus 7:3

moyo wa Farao mgumu

Hapa "moyo" wa husu Farao. Tabia yake ya kiburi inazungumziwa kama moyo mgumu.

ishara nyingi ... maajabu mengi

Maneno "ishara" na "maajabu" yana maana moja. Mungu anatumia kukazia ukuu wa atakayo ya fanya Misri.

nitaueka mkono wangu juu ya ... nyoosha mkono wangu kwa

Maneno "mkono wangu" ya wakilisha nguvu kubwa ya Mungu.

Exodus 7:6

na miaka themanini na tatu

"na Aruni alikuwa na miaka themanini na tatu

Exodus 7:8

Wakati Farao atakapo waambia, 'Fanya muujiza,' utamwambia Aruni, 'Chukuwa gongo lako na ulirushe chini mbele ya Farao, ililigeuke nyoka

Hii yaweza andikwa kama nukuu isiyo ya moja kwa moja.

Exodus 7:11

lilimeza

"lilikula" au "liliharibu"

Moyo wa Farao ulikuwa mgumu

Hapa "moyo" wa husu Farao. Tabia yake ya kiburi inazungumziwa kama moyo wake ulikuwa mgumu.

Exodus 7:14

Moyo wa Farao ni mgumu

Hapa "moyo" wa husu Farao. Tabia yake ya kiburi ya zungumziwa kama moyo wake ulikuwa mgumu.

anapoenda kwenye maji

Maana kamili ya sentesi yaweza fanya halisi.

Exodus 7:16

Mwambie

"Sema kwa Farao"

piga maji

"gonga maji"

Exodus 7:19

nzima

"kila sehemu"

Exodus 7:20

moyo wa Farao ukawa mgumu

Hapa "moyo" wa husu Farao. Tabia yake ya kiburi ya zungumziwa kama moyo mgumu.

kwenye mto

Jina la mto la weza fanywa alisi.

Exodus 7:23

Wamisri wote

Neno "wote" hapa la ni msisitizo wa kukazia jinsi tatizo lilivyo kuwa kubwa.

Exodus 8

Exodus 8:1

Mto

"Mto Nile"

vyombo vya kukandia mkate

Hivi ni vyombo vya mkate watengenezewa

Exodus 8:8

Kisha Farao akawaita Musa na Aruni

"Kisha Farao akawatuma Musa na Aruni"

Unaweza chukuwa fursa ya kuniambia lini nikuombee wewe

"Unaweza chagua lini ni kuombee wewe" au "Unaweza chagua muda wa kukuombea"

Exodus 8:13

aliufanya moyo wake kuwa mgumu

"Farao akaufanya moyo wake mgumu." Hapa "mgumu" ya maanisha akawa na kiburi.

kama Yahweh alivyo sema

"kama Yahweh alivyo sema Musa ata fanya"

Exodus 8:18

Hichi ni kidole cha Mungu

Maneno "kdiole cha Mungu" ya wakilisha nguvu ya Mungu.

moyo wa Farao ulikuwa Mgumu

Hapa "moyo" wa husu Farao.

Exodus 8:20

usimame mbele ya Farao

"jiwakilishe kwa Farao"

Acha watu wangu waende

"waeke watu wangu huru"

Exodus 8:22

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuzungumza na Farao kupitia Musa.

nchi iliharibiwa na makundi ya nzi

Hii yaweza tafsiriwa katika tensi tendaji.

Exodus 8:25

mbele ya macho yao

Hii ilikuwa desturi ya kusema "mbele ya uwepo wa mtu"

hawata tupiga mawe?

Musa ana uliza hili swali kumuonyesha Farao kuwa Wamisri wata waruhusu Waisraeli kumuabudu Yahweh.

Exodus 8:28

usifanye udhalimu tena kwa kutowaacha watu wetu waende

Hii yaweza andikwa katika mfumo halisi.

Lakini usifanye udhalimu

"Lakini husitudanganye sisi"

Exodus 8:30

Farao aliufanya moyo wake mgumu

Hapa "moyo" wa husu Farao.

Exodus 9

Exodus 9:1

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuzungumza na Musa kuhusu kushughulika na Farao na kuwaleta watu Waebrania njee ya Misri.

ukikataa kuwaruhusu waende, kama utaendelea kuwa bakiza nyuma

Hii mistari miwili ina maana moja. Watamsisitiza Farao nini kitakacho watokea Farao akifanya hivi.

basi mkono wa Yahweh utakuwa kinyume dhidi

Neno "mkono" hapa wa wakilisha nguvu ya Yahweh ya kuwa dhuru wanyama kwa magonjwa.

ya mifugo yako

Neno "yako" hapa la husu watu wote wa Misri waliyo miliki mifugo.

mifugo ya Israeli

Hapa "Israeli" ya husu watu wa Israeli.

mifugo Misri

Neno "Misri" hapa la husu watu wa Misri

Exodus 9:5

ametenga muda

"ameeka muda" au "ameandaa muda"

mifugo yote ya Misri ikafa

Hii iwe ongezewa kukazia umakini wa tukio.

mifugo ya Misri

Hapa "Misri" ya husu watu wa Misri.

Farao akafanya utafiti

Farao akakusanya ukweli kuhusu hali.

tazama

Neno "tazama" hapa laonyesha kwamba Farao alishangazwa kwa alicho kiona.

moyo wake ulikuwa mjeuri

Hapa "moyo" wa husu Farao.

Exodus 9:8

tanuru

"shimo la moto"

safi

"kidogo sana"

kutokea kwa

"kutokea kwa haraka kwa watu"

Exodus 9:11

Yahweh akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu

Hapa "moyo" wa husu Farao. Tabia yake ya kiburi inazungumzwa hapa kama moyo wake mgumu.

Exodus 9:13

kwako wewe

Hii ina maana kuwa ata Farao ata umizwa kwa mapigo.

Nitafanya hivi ili ujue

Neno "hivi" la husu mapigo ambayo Musa alimwambia Farao kuhusu.

Exodus 9:15

ningeweza kuunyosha mkono wangu na kukushambulia wewe

Hapa "mkono wangu" wa husu nguvu ya Mungu.

ili kwamba jina langu litangazwe dunia nzima

Hapa "jina langu" la wakilisha sifa ya Yahweh.

unajiinua dhidi ya watu wangu

Upinzani wa Farao kuto waachia wa Israeli kwenda kumuabudu Yahweh unazungumziwa kama anajiinua yeye kuwa kikwazo kwao.

Exodus 9:18

Sikiliza!

"Kuwa makini kwa kitu muhimu ninacho kuambia"

Exodus 9:27

waite

"kuita"

Exodus 9:29

Musa akamwambia

"Musa akasema kwa Farao"

nitaitanua mikono yangu kwa Yahweh

Hili tendo la ishara la ambatana na maombi.

mheshimu Yahweh Mungu

Kumheshimu Mungu kwa husu kumtii na kuishi kwa namna inayoonyesha jinsi alivyo mkuu.

Exodus 9:31

kitani

Huu ni mmea unao zalisha nyuzi zinazo tengeneza nguo.

shayiri

Hii ni aina ya mbegu inayo tumika kutengeneza mkate; pia ya tumika kulisha mifugo.

kusemethu

Hii ni aina ya ngano

alitanua mikono yake kwa Yahweh

Hii ishara ya ambatana na maombi

Exodus 9:34

kufanya moyo wake kuwa mgumu

Hapa "moyo" wa husu Farao. Tabia yake ya kiburi inazungumzwa hapa kama moyo wake mgumu.

Moyo wa Farao ulikuwa mgumu

Hapa "moyo" wa husu Farao. Tabia yake ya kiburi inazungumzwa hapa kama moyo wake mgumu.

Exodus 10

Exodus 10:1

nimeufanya moyo wake mgumu na moyo wa watumishi wake

Yahweh anazungumza kuhusu kumfanya Farao na watumishi wake kuwa na kiburi kama alikuwa anafanya mioyo yao migumu.

tofauti

"aina mbali mbali"

Exodus 10:3

sikiliza

Hili neno la tilia mkazo kwa alicho sema mbeleni

Exodus 10:5

mvua ya barafu ya mawe

mvua ya barafu ya mawe ni mtone ya mvua yanayo ganda mawinguni.

halikuwai shuhudiwa

Hii yaweza wekwa katika tensi tendaji.

Exodus 10:7

msumbufu

Mtu "msumbufu" ni mtu anaye leta shida au madhara.

Mpaka lini huyu mwanaume ata kuwa msumbufu kwetu?

Watumishi wa Farao wanauliza hili swali kumuonyesha Farao kiasi cha uharibifu wa Misri.

Bado haujatambua kuwa Misri imeharibiwa?

Watumishi wa Farao wanauliza hili swali kumleta Farao atambue anacho kataa kuona.

Misri imeharibiwa

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 10:9

kama nitawaacha muende na wadogo zenu waende

Farao anasema hivi kukazia kwamba hata muacha Musa awachukuwe watoto kwenda muabudu Yahweh.

Kisha Musa na Aruni wakaondolewa uweponi mwa Farao

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 10:14

ikawa giza

kulikuwa na nzige wengi nchi ikaonekana kuwa giza. Kisha hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 10:16

wakati huu

"mara ingine tena"

aondoe hichi kifo kwangu

Neno "kifo" hapa la eleza uharibifu wa nzige kwa mimea yote Misri, ambayo hatimae itapelekea vifo vya watu kwasababu hakuna mazao. Maana yote ya hii sentesi yaweza andikwa kwa uhalisi.

Exodus 10:19

wachukuwa wale nzige

"kuwapeleka nzige juu"

Yahweh aliufanya moyo wa Farao mgumu

Hapa "moyo" wa husu Farao. Tabia yake ya kiburi inazungumzwa hapa kama moyo wake mgumu.

Exodus 10:21

giza linalo weza kuhisiwa

Yahweh anazungumzia giza lililo pitiliza kana kwamba ni nene sana hadi watu wanaweza shika mikononi mwao. Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 10:24

ata mmoja hawezi kubaki

Hapa "ata mmoja" ya husu wanyama wote. Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 10:27

Yahweh aliufanya moyo wa Farao mgumu

Hapa "moyo" wa husu Farao. Tabia yake ya kiburi inazungumzwa hapa kama moyo wake mgumu.

hakuwaacha waende

"Farao hakuwaacha waende"

Kuwa muangalifu na jambo moja

"Hakikisha jambo moja" au "Kuwa na uhakika kuhusu jambo moja"

uona uso wangu

Hapa neno "uso" la husu mtu wote"

Wewe mwenyewe umesema

Kwa haya maneno, Musa anakazia kuwa Farao amesema ukweli.

Exodus 11

Exodus 11:1

atakuacha uondoke hapa

Kila muonekano wa neno "ataku" katika huu mstari ni katika wingi na la husu Musa na Waisraeli wote.

Exodus 11:4

manane

Huu ni muda kati ya saa 6 usiku

Wazaliwa wa kwanza ... mzaliwa wa kwanza wa Farao ... mzaliwa wa kwanza wa misichana mtumwa ... wazaliwa wa kwanza wa mifugo

"Mzaliwa wa kwanza" mara zote wa husu mzao mkubwa wa kiume.

anaye keti kiti chake cha enzi

Hii ya husu Farao

anaye saga mbegu

"anaye saga katika jiwe la kusagia"

Exodus 11:6

Baada ya hapo nitaondoka

Hii ina maana ya kuwa Musa na watu wa Israeli wataondoka Misri.

Exodus 11:9

Yahweh aliufanya moyo wa Farao mgumu

Hapa "moyo" wa husu Farao. Tabia yake ya kiburi inazungumzwa hapa kama moyo wake mgumu.

Exodus 12

Exodus 12:1

Kwako wewe, mwezi huu utakuwa mwanzo wa miezi, mwezi wa kwanza wa mwaka kwako

Hii mistari miwili ina maana moja na kukazia kuwa mwezi ambao haya matukio yana tokea ndio utakuwa mwanzo wa mwaka wa wao wa kalenda.

mwezi wa kwanza wa mwaka

Mwezi wa kwanza wa kalenda ya Kiebrania ya jumuisha sehemu ya mwisho ya Machi na sehemu ya kwanza ya Aprili katika kalenda za Magharibi. Ina weka alama wakati Yahweh alipo waokoa Waisraeli kutoka Misri.

Exodus 12:3

Kama hiyo nyumba ni ndogo sana kwa mwana kondoo

Hii ina maana hakuna watu wakutosha katika familia kula mwana kondo mzima.

mwanaume na jirani yake

Hapa "mwanaume" ya husu mwanaume aliye kiongozi wa familia.

Exodus 12:5

jioni

Hii ya husu muda wa jioni baada ya jua kuzama lakini bado pakiwa na mwanga.

kwenye sehemu mbili za mihimili ya milango na juu ya fremu za milango

"pembeni na juu ya njia ya kuingia"

Kula na mkate ulio andaliwa kwa hamira

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

mimea michungu

Haya ni majani madogo yenye ladha kali na mbaya.

Exodus 12:9

Usiile mbichi

"Usile mwana kondo au mbuzi bila kupika"

Usiache ata kidogo kubaki mpaka asubui

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

mkanda

Hii ya husu mshipi wa ngozi au kitambaa cha kufunga kiunoni.

ule kwa haraka

"kula kwa haraka"

Ni Pasaka ya Yahweh

Hapa neno "ni" la husu kula mnyama siku ya kumi ya mwezi.

Exodus 12:12

Nitaleta pigo kwa miungu yote ya Misri.

Hii yaweza andikwa katika kwa tensi nenaji

ya kuja kwangu

Hii ya hashiria kwamba Yahweh ataona damu ambayo yaonyesha nyumba ya Misraeli.

nitapita

Neno "kupita" ilikuwa desturi ya kusema husitembelee au kuingia.

kwenu pia, kwenye vizazi vyote vya watu wenu

"kwako wewe na vizazi vyote vya uzao wako"

Exodus 12:15

huyo mtu lazima akatwe kutoka Israeli

Mafumbo "akatwe" ina maana kama tatu zinazo wezekana. Inaweza elezewa katika tensi tendaji: 1)"watu wa Israeli lazima wamuondoe" au 2) "sitamuhesabu kuwa mmoja wa watu wa Israeli" au 3) "watu wa Israeli lazima wamuue"

kusanyiko lililo tengwa kwa ajili yangu

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Hakuna kazi itakayo fanywa hizi siku

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Hiyo ndio kazi pekee itakayo fanywa na wewe

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 12:17

makundi yaliyo na silaha, kwa makundi yaliyo na silaha

Neno lilotumika kwa haya makundi ni neno la kijeshi ikimaanisha idadi kubwa ya wanajeshi.

jiono

Hii ina maana ya muda ambao jua limezama wakati bado kuna mwanga.

siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza

Huu ni mwezi wa kwanza wa kalenda ya Kiebrania. Siku ya kumi na nne ni karibu na mwanzo wa Aprili katika Kalenda za Magharibi.

siku ya ishirini na moja ya mwezi

siku ya ishirini na moja ya mwezi wa kwanza. Hii ni karibu na katikati ya Aprili kwa Kalenda za Magharibi.

Exodus 12:19

nyumbani mwenu kusipatikane na hamira

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

lazima akatwe kutoka jamii ya Israeli

Mafumbo "akatwe" ina maana kama tatu zinazo wezekana. Inaweza elezewa katika tensi tendaji: 1)"watu wa Israeli lazima wamuondoe" au 2) "sitamuhesabu kuwa mmoja wa watu wa Israeli" au 3) "watu wa Israeli lazima wamuue"

mkate usio na hamira

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji

Exodus 12:21

waita

"kuwaita rasmi"

hisopu

Huu ni mmea katika jamii ya mnaa,

juu ya fremu ya mlango na kwenye mihimili miwili ya mlango

"pembeni na juu ya njia ya kuingia nyumbani"

Exodus 12:23

atapita mlango wako

Hapa neno "mlango" una maana ya nyumba nzima. Hii ina maana kwamba Mungu ata wanusuru Waisraeli wenye damu mlangoni.

Exodus 12:24

hili tukio ... hili tendo la ibada

Hii mistari ya husu Pasaka au Sherehe ya Mikate isiyo tiwachachu. Kuadhimisha Pasaka ilikkuwa tendo la kumuabudu Yahweh.

Exodus 12:26

Aliweka nyumba zetu huru

Hii ina maana kwamba Yahweh alinusuru wana wa kwanza wa kuzaliwa wa Waisraeli.

kama Yahweh alivyo waamuru Musa na Aruni

"kila kitu Yahweh alicho mwambia Musa na Aruni kufanya"

Exodus 12:29

usiku wa manane

"katikati ya usiku"

wazaliwa wote wa kwanza wa nchi ya Misri

Hapa "wazaliwa wa kwanza" mara zote ina maana ya mzao mkubwa wa kiume.

aliye keti kiti chake cha enzi

Hii ya husu Farao.

mzaliwa wa kwanza wa mtu aliye gerezani

Hii ya husu wafungwa, kwa ujumla, na sio mtu maalumu gerezani.

Palikuwa na kelele za maombolezo Misri

Hii yaweza andikwa katika tensi nenaji.

kwa kuwa hakukuwa na nyumba ambayo hamna mtu hakufa

Hii hasi mbili ina sisitiza chanya.

Exodus 12:31

Sisi ni watu tuliokufa

Wamisri wanatumia tensi endelevu kusisitiza kuwa watakufa hakika kama Waisraeli hawata ondoka Misri.

Exodus 12:34

Bakuli zao zakukandia ngano zilifungiwa kwenye nguo zao na kwenye mabega yao

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 12:37

Ramesi

Ramesi ulikuwa mji mkuu sana Misri ambapo mbegu zilihifadhiwa.

Walikuwa na idadi ya wanaume 600,000

"Idadi ya jumla ya wanaume ilikuwa 600,000"

waliondolewa Misri

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 12:41

majeshi yote ya Yahweh yalio jiami

Hii ina husu makabila ya Israeli.

kuadhimishwa na Waisraeli wote

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Waisraeli wote na watu wa vizazi vyao vyote

"Waisraeli wote na vizazi vya uzao wao"

Exodus 12:43

hakuna mgeni anaye ruhusiwa kuila

"kuila" ina husu chukula cha Pasaka.

kila mtumwa wa Misraeli

"mtumwa yeyote wa Muisraeli"

nunuliwa kwa pesa

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 12:45

Chakula chapaswa kuliwa ndani ya nyumba moja

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 12:47

ndugu zake wote wa kiume wapaswa kutahiriwa

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

watu walio zaliwa kwenye nchi

Hapa neno "nchi" ya husu Kanani. Msemo "walio zaliwa katika nchi' ina maana ya Misraeli halisi.

hakuna mtu asiye tahiriwa anaruhusiwa kula

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 12:49

kama Yahweh alivyo waamuru Musa na Aruni.

"kila kitu Yahweh alicho mwambia Musa na Aruni kufanya"

Ikaja kuwa

Huu mstari unatumika hapa kuweka alama ya tukio muhimu katika adithi.

kwa makundi yalio jiami

Neno lilotumika kwa haya makundi ni msemo wa kijeshi unao husu idadi kubwa ya wanajeshi.

Exodus 13

Exodus 13:1

Nitengee ... kila mzaliwa wa kwanza

Mungu anataka kila mzaliwa wa kwanza wa kiume atengwe kwa ajili yake.

Exodus 13:3

kumbukeni hii siku,

Hii ilikuwa ni namna ya kidesturi ya kumwambia mtu azingatie.

nyumba ya utumwa

Musa anazungumzia Misri kama nyumba watu wanapo hifadhia watumwa.

mkono hodari wa Yahweh

Hapa neno "mkono" ya husu nguvu.

Hakuna mkate wa hamira waruhusiwa kuliwa

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

mwezi wa Abibu

Hili ni jina la mwezi wa kwanza wa kalenda ya Kiebrania. Abibu ni wakati wa sehemu ya mwisho ya Machi na sehemu ya kwanza ya Aprili kwa kalenda za Magharibi.

nchi inayo tiririka kwa maziwa na asali

Tangu maziwa yanatoka kwa ng'ombe na mbuzi, "maziwa" uwakilisha chakula kizalishwacho na mifugo. Kwasababu asali utengenezwa na maua, "asali" uwakilisha chakula cha mazao.

wapaswa kuadhimisha hili tendo la ibada

Wakati Waisraeli watakapo ishi Kanani, lazima wa shereheke Pasaka hii siku kila mwaka.

Exodus 13:6

Maelezo ya Jumla

Musa anaendelea kuongea na watu wa Israeli.

Kwa siku saba

"Kwa siku 7"

Mkate usio na hamira wapaswa kuliwa

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

hakuna mkate ulio na hamira wapaswa kuliwa miongoni mwenu

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Hakuna hamira yapaswa kuonekana

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

kwenye mipaka yenu

"katika mipaka yenu yeyote ya nchi"

Exodus 13:8

Hiyo siku utasema kwa watoto wako, 'Hii ni kwasababu ya kile Yahweh alichofanya kwangu nilipo taka Misri.'

Nukuu yaweza kwa namna isiyo ya moja kwa moja.

Hii itakuwa kumbukumbu mkononi mwako, na kumbukumbu kwenye paji la uso wako

Hii ni kumbukumbu mbili za mwilini ili watu wasisahau kitu muhimu.

kumbukumbu mkononi mwako

Musa anazungumza kuhusu kusherehekea siku kuu kana kwamba inafunga kitu mikononi mwao kuwakumbusha nini Yahweh amefanya.

kumbukumbu kwenye paji la uso wako

Musa anazungumza kuhusu kusherehekea siku kuu kana kwamba inafunga kitu mikononi mwao kuwakumbusha nini Yahweh amefanya.

ili sheria ya Yahweh iwe kinywani mwako

Maneno "kinywani mwako" hapa ya husu maneno wanayo sema.

mkono hodari

Neno "mkono hapa wa wakilisha matendo ya Mungu au kazi.

Exodus 13:11

na atakapo wapa nchi ninyi

"na atakapo wapa nchi ya Wakanani ninyi"

Kila mzaliwa wa kwanza wa punda

Israeli inapewa uchaguzi wa kuua mzaliwa wa kwanza wa punda au kumnunua tena kwa mwana kondoo.

kila mzaliwa wa kwanza wakiume miongoni mwenu

Kila mtu Israeli aliye kuwa na mwana wa kwanza kuzaliwa, lazima amnunue tena.

Exodus 13:14

Mwanae atakapo kuuliza baadae, 'Hii ina maana gani?' kisha utamwambia

Nukuu ya kwanza yaweza andikwa kama nukuu isiyo ya moja kwa moja.

mkono hodari

Neno "mkono" hapa ya wakilisha matendo ya Mungu au kazi.

nyumba ya utumwa

Musa ana i zungumzia Misri kama ni nyumba watu wana hifadhia watumwa.

kumbukumbu mikononi mwako na kumbukumbu kwenye paji lako la uso

Hii ni kumbukumbu mbili ili watu wasisahau kitu muhimu.

Exodus 13:17

karibu

"karibu na eneo walilo kuwepo"

watu watabadili nia zao ... na ... watarudi Misri

Tangu Waisraeli waliishi utumwani maisha yao yote, walizoea amani zaidi ya vita na radhi wa rudi utumwani kuliko kupigana.

Exodus 13:19

kuweka kambi Ethamu

Ethamu ipo kusini mwa njia ya kuelekea kwa Wafilisti, katika mpaka wa nyikani.

nguzo ya wingu ... nguzo ya moto

"wingu kwa mfumo wa mnara ... moto kwa mfumo wa mnara." Mungu yupo nao kwa wingu mchana na moto usiku.

Exodus 14

Exodus 14:1

Pi Hahirothi ... Migdoli ..Baali Zefoni

Hii ni miji ya mashriki ya mipaka ya Misri.

Wapaswa kueka kambi

Hapa neno "wapaswa" ni wingi na la husu Musa na Waisraeli.

Farao atasema kuhusu Waisraeli, 'Wanaangaika kwenye nchi. Nyikani imewafunika.'

Hii ya weza andikwa kama nukuu isiyo ya moja kwa moja.

Nyikani imewafunika

Farao anaingelea nyikani kama mtu aliye wakamata Waisraeli.

Exodus 14:4

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwelekeza Musa wapi pa kwenda na nini Yahweh atafanya.

Nitaufanya moyo wa Farao mgumu

Hapa "moyo" wa husu Farao. Tabai yake ya kiburi inazungumziwa kama moyo wake ni mgumu.

yeye ata wakimbiza

"Farao ata wakimbiza Waisraeli"

Nitapata utukufu

"Watu watani heshimu"

Wamisri watajua mimi ni Yahweh

"Wamisri wataelewa kwamba mimi ni Yahweh, Mungu mmoja wa kweli"

Kisha Waisraeli wakaeka kambi kama walivyo elekezwa

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Mfalme wa Misri alipo ambiwa

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Mfalme wa Misri

Hii ya husu Farao.

wametoroka

"wamekimbia"

, nia ya Farao na watumishi wake ikageuka dhidi ya watu

Hapa neno "nia" ya husu tabia zao kwa Waisraeli.

Tumefanya nini kwa kuwaacha Waisraeli waende huru na wasitutumikie?

Waliuliza hili swali wakidhani kuwa wamefanya kitu cha kijinga.

Exodus 14:6

Alichukuwa magari ya farasi mia sita imara

"Alichukuwa magari yake ya farasi 600 bora"

Yahweh akafanya mgumu moyo wa Farao

Hapa "moyo" wa husu Farao. Tabia yake ya kiburi inazungumizwa kama moyo wake mgumu.

Pi Hahirothi ... Baali Zefoni

Hii miji mashariki mwa mipaka ya Misri.

Exodus 14:10

Farao alipo kuja karibu

Neno "Farao" hapa ya wakilisha jeshi lote la Misri.

waliogopa

"Waisraeli waliogopa"

Ni kwasababu hakukuwa na makaburi Misri, hadi umetuleta tufe huku nyikani?

Waisraeli wanauliza hili swali kuonyesha uchovu wao hofu ya kufa.

Kwanini umetutendea hivi, kwa kututoa Misri?

Waisreali wanauliza hili swali kumkemea Musa kwa kuwaleta kwenye jangwa kufa.

Hili si ndilo tulilo kwambia Misri?

Waisreali wanauliza hili swali kusisitiza kwamba hili ndilo walillo mwambia Musa.

Tulikwambia, 'Utuache, ili tuwafanyie Wamisri kazi.'

Hii yaweza andikwa kama nukuu isiyo ya moja kwa moja.

Exodus 14:13

Musa akawaambia watu

Musa anajibu hofu za Waisraeli.

atakao uleta kwenu

"kwenu" ya husu Waisraeli wote

Kwa maana hamtawaona tena Wamisri

Musa alitumia lugha ya busara kusema Mungu anaenda kuangamiza jeshi la Wamisri.

Exodus 14:15

Kwanini wewe, Musa, unaendelea kuniita mimi?

Musa ni wazi alikuwa akiomba kwa Mungu kwa msaada hivyo Mungu anatumia hili swali kumshawishi Musa kutenda.

uigawanye sehemu mbili

"gawanya bahari katika sehemu mbili"

Jitahadharishe

"jua"

nitafanya mioyo ya Wamisri kuwa migumu

Hapa "mioyo" ya husu Wamisri wenyewe. Tabia zao za kiburi zinatajwa kama mioyo yao migumu.

ili wawafuate

"ili kwamba Wamisri wataenda kwenye bahari baada ya Waisraeli"

Exodus 14:19

kambi ya Misri na kambi ya Israeli

"jeshi la Wamisri na watu wa Israeli"

hivyo upande mmoja haukuweza kuja karibu ya mwingine

Hii ina maana kuwa Wamisri na Waisraeli hawakuweza fikiana.

Exodus 14:21

upepo mkali wa mashariki

Upepo wa mashariki watoka mashariki na wapiga magharibi.

mashariki

jua linapo chomoza

maji yaligawanyika

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

mkono wao wa kulia na mkono wao wa kushoto

"kila upande wao" au "pande zao mbili"

Exodus 14:23

Alisababisha hofu miongoni mwa Wamisri

Hofu ni pale mtu anapo ogopa hadi hawezi fikiri kawaida.

Magari yao ya farasi yalikuwa yana kwama matairi

Hii yaweza anadikwa katika tensi tendaji.

Exodus 14:26

Yahweh akamwambia Musa, "Nyoosha mkono ... na wapanda farasi wao."

Hii yaweza andikwa kama nukuu isiyo ya moja kwa moja.

yawarudie

"kuwaangukia"

Wamisri walikimbilia ndani ya bahari

Tangu bahari ilikuwa inafunga juu ya Wamisri, badala ya kutoroka, walikuwa wanakimbia ndani ya maji.

Yahweh akawaingiza Wamisri

"Yahweh akawasukuma Wamisri" au "Yahweh akawatupa Wamisri"

Exodus 14:29

Israeli

Kila tokeo la "Israeli" ya husu watu wa Israeli.

kutoka mkono wa Wamisri

Hapa neno "mkono" ya husu nguvu.

ufukweni

"katika nchi kando ya bahari"

Exodus 15

Exodus 15:1

Maelezo ya Jumla

Huu ni wimbo wa matukio yaliyo tokea 14:16

farasi na dereva wake amewatupa kwenye bahari

Musa aliimba kuhusu Mungu kusababisha bahari kufunika na kuzamisha farasi na dereva kana kwamba Mungu kawatupa baharini.

farasi na dereva wake

Hii inahusu wote au farasi wengi wa Wamisri na madereva waliyo kuwa wakiwafukuzia Waisraeli.

dereva

Huyu ni mtu anaye keti kwenye farasi au ana safiri kwa gari la farasi linalo vutwa na farasi.

Exodus 15:2

Yahweh ni uweza wangu

Maana zinazo wezekana ni 1) "Yahweh ndiye anaye nipa uweza" au 2) "Yahweh ndiye mwenye nguvu anaye ni linda mimi."

na nyimbo

Musa anamuita Yahweh nyimbo yake kwasababu Yahweh ndiye anaye imba kuhusu.

amekuwa wokovu wangu

Musa anamuita Mungu wakovu wake kwasababu Mungu amemuokoa.

Yahweh ni shujaa

Musa anamuita Mungu shujaa kwasababu Mungu kwa nguvu alipigana dhidi ya Wamisri na kushinda.

Exodus 15:4

Ametupa magari ya farasi ya Farao na jeshi lake kwenye bahari

Musa anaimba kuhusu Mungu kusababisha bahari kufunika magari ya Farao na jeshi kana kwamba Mungu amewatupa baharini.

walienda kwenye kina kama jiwe

Kama jiwe lisivyo elea lakini la zama chini ya bahari, majeshi ya maadui yamezama chini ya bahari.

Exodus 15:6

Mkono wako wakulia, Yahweh, una nguvu ya utukufu

Musa anamzungumzia Mungu kama Mungu ana mikono. Mkono wa kulia wa husu nguvu ya Mungu au vitu Mungu anavyo fanya kwa nguvu.

mkono wako, Yahweh, umewavunja adui

Musa anamzungumzia Mungu kama Mungu ana mikono. Mkono wa kulia wa husu nguvu ya Mungu.

umewavunja adui

Musa anazungumzia adui kana kwamba ni dhahifu na waweza vunjwa kama kio au chungu.

walio inuka dhidi yako

Kuasi dhidi ya Mungu kuna zungumziwa kama kujiinua dhidi yake.

Umetuma gadhabu

Musa anazungumzia gadhabu ya Mungu kana kwamba ni mtumishi aliye mtuma kufanya kitu

imewateketeza kama karatasi

Musa anazungumzia gadhabu ya Mungu kana kwamba ni moto unao weza kuchoma vitu. Maadui zake waliharibiwa kabisa kama karatasi.

Kwa pumzi ya pua yako

Musa anamzungumzia Mungu kana kwamba Mungu ana pua, na upepo kana kwamba Mungu kapuliza upepo kwa kutoka puani mwake.

Exodus 15:9

tamanio langu litatimizwa kwao

Hii yaweza elezwa katika tensi tendaji.

mkono wangu utawaharibu wao

Maadui wanaongea kuwaharibu Waisraeli kwa nguvu ya mkono wao kana kwamba ni mikono itakyo waharibu.

Lakini ulipuliza kwa upepo wako

Musa aliongea kuhusu Mungu kufanya upepo upulize kana kwamba Mungu alipuliza upepo kupitia pua au mdomo.

walizama kama chuma nzito kwenye maji mengi

Chuma ni kifaa kizito kinacho tumika kawaida kufanya vitu vizame majini. Neno "chuma" linatumika hapa kuonyesha jinsi Mungu alivyo haribu maadui zake.

Ni nani kama wewe, Yahweh, miongoni mwa miungu?

Musa anatumia hili swali kuonyesha jinsi alivyo mkuu.

Nani kama ... fanya miujiza?

Musa anatumia hili swali kuonyesha jinsi alivyo mkuu.

Exodus 15:12

mkono wako wa kulia

Maneno "mkono wakulia" ya wakilisha nguvu kuu ya Mungu.

Ulinyoosha mkono wako wa kulia

Musa anaongea kuhusu Mungu kusababisha kitu kitokee kana kwamba Mungu alinyoosha mkono wake.

dunia ikawameza

Musa ana nafsisha dunia kana kwamba inaweza kumeza au kurarua kwa mdomo wake.

Exodus 15:14

tetemeka

Hii ina maana kutikisika kwasababu una ogopa.

hofu itawakumba wakazi wa Filistia

Musa anaongelea hofu kana kwamba ni mtu anaye weza kuchukuwa kwa nguvu mtu na kumfanya aogope sana.

watayayuka

Musa anaongelea watu kuwa wadhaifu kutokana na hofu ya kuyayuka.

Exodus 15:16

Sentensi Unganishi

Musa anaendelea kuimba kuhusu jinsi watu wa mataifa mengine watajisikia watakapo waona watu wa Mungu.

Mshituko na hofu vitawaangukia

Haya maneno mawili yana maana hofu itakuja juu yao.

hofu

Hofu ni uwoga au wasiwasi kuhusu kitu kinachoenda tokea au kilicho tokea.

Kwasababu ya nguvu ya mkono wako

Mkono wa Mungu wa wakilisha uweza wake mkuu.

watakuwa kimya kama jiwe

Maana zinazo wezekana ni 1) "Watakuwa tulivu kama jiwe" au 2) "Hawata sogea kama jiwe"

Exodus 15:17

Utawaleta

Pale Mungu atakapo waleta yaweza andikwa wazi. Tangu Musa bado hakuwa Kanani, baadhi ya lugha zitatumia "chukuwa" badala ya "leta"

kuwapanda kwenye mlima

Musa anaongelea kuhusu Mungu kuwapa watu wake nchi ya kuishi kana kwamba wao ni mti ambao Mungu anaupanda.

mlima wa urithi wako

Hii ya husu Mlima Sayuni katika nchi ya Kanani.

wa urithi wako

Musa anaongelea kuhusu Mungu kuahidi kuwapa watu mlima milele kana kwamba alikuwa anawapa urithi.

mikono yako iliyo jenga

Maneno "mikono yako" ya husu nguvu ya Mungu.

Exodus 15:19

Miriamu .. Aruni

Miriamu alikuwa dada wa kwanza wa Musa na Aruni.

tari

Hichi ni chombo cha muziki kama ngoma ndogo yenye vipande vya chuma pembeni vinavyo toa sauti vikitikizwa

ameshinda kwa utukufu

"ameshinda kwa utukufu juu ya maadui zake"

Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini

Musa aliimba kuhusu Mungu kusababisha bahari kufunika na kuzamisha farasi na madereva kana kwamba Mungu aliwatupa baharini.

Exodus 15:22

Musa akaongoza Israeli

Neno "Israeli" la wakilisha watu wa Israeli.

nyikani ya Shuri ...Mara

Hatujui maeno ya hizi sehemu.

Exodus 15:24

wakamlalamikia Musa na kusema

"hawakufurahi na kumwambia Musa" au "kwa hasira wa kamwambia Musa"

sauti ya Yahweh Mungu wako

Yahweh anazungumza kuhusu sauti yake.

kufanya yalio sahihi machoni pake

Maneno "machoni pake" hapa ya wakilisha kile Mungu alicho amini au kuamua.

sitawaekea ninyi magonjwa

Mungu anaongea kusababisha watu kuwa na magonjwa kam kuweka magonjwa juu yao.

Exodus 15:27

Elimu

Hii ni sehemu ya mapumziko jangwani, sehemu yenye maji na vivuli vya miti.

kumi na mbili

"12"

sabini

"70"

Exodus 16

Exodus 16:1

nyikani mwa Sinu

Neno "Sinu" hapa ni jina la Kiebrania la nyikani. Sio neno la kiengereza lenye maana ya "dhambi"

siku ya kumi na tano ya mwezi wa pili

Huu muda unaingiliana na mwisho wa Aprili na mwanzo wa Mei katika kalenda za Magharibi.

Jamii yote ya Waisraeli

"Waisraeli woe" Huu ni ujumla. Musa na Aruni hawakulalamika.

lalamika

"walikuwa na hasira na kusema"

Kama tu tungekufa

Hii ni namna ya kusema wangetamani kufa.

kwa mkono wa Yahweh

Manaeno "mkono wa Yahweh" wa wakilisha matendo ya Yahweh.

Exodus 16:4

Nitakunyeshea mvua ya mkate.

Mungu anaongelea chakula kutoka mbinguni kana kwamba ni mvua.

mkate

Mungu anaongelea chakula ambacho atakituma kana kwamba ni mkate. Waisraeli watakula hichi chakula kila siku, kama walivyo kula mkate kila siku kabla ya hichi.

wataendelea kushika sheria yangu

Mungu anaongelea kutii sheria yake kama kutembea ndani yake.

sheria yangu

"amri yangu"

Itakuja kuwa siku ya sita, kwamba wata

"itatokea siku ya sita kwamba wata" au "siku ya sita wata"

siku ya sita

"siku ya 6"

Exodus 16:6

Sisi ni nani hadi mtulalamikie?

Musa na Aruni walitumia hili swali kuonyesha watu kwamba ilikuwa ni upumbavu kuwalalamikia wao.

mkate

Mungu anaongelea chakula ambacho atakituma kana kwamba ni mkate. Waisraeli watakula hichi chakula kila siku, kama walivyo kula mkate kila siku kabla ya hichi.

Nani ni Aruni na mimi?

Musa anatumia hili swali kuwaonyesha watu kuwa yeye na Aruni hawakuwa na nguvu yakuwapa walicho taka.

Malalamishi yenu sio dhidi yetu; ni dhidi ya Yahweh

Watu walikuwa wana lalamika dhidi ya Musa na Aruni, ambao walikuwa watumishi wa Yahweh. Hivyo kwa kulalamika dhidi yao, watu kihalisi walikuwa wana lalamika dhidi ya Yahweh.

Exodus 16:9

Ikawa

Hili neno linatumika kuweka alama ya tukio muhimu katika historia. Tukio muhimu hapa ni watu kuona utukufu wa Yahweh.

tazama

Neno "tazama" hapa la onyesha kwamba watu waliona kitu cha kuvutia.

mkate

Mungu anaongelea chakula ambacho atakituma kana kwamba ni mkate. Waisraeli watakula hichi chakula kila siku, kama walivyo kula mkate kila siku kabla ya hichi.

Exodus 16:13

Ikaja kuwa kwamba

Hili neno linatumika kuweka alama ya tukio muhimu.

kware

Hawa ni ndege wadogo na wanene.

kama barafu

Wasomaji wa mwanzo walijua barafu ilivyo kuwa, hivyo neno hili litawasaidia kuelewa nini hiyo theluji ilivyo kuwa. Theluji ni umande ulio ganda unao undika kwenye ardhi. Ni nyeupe sana.

mkate

Mungu anaongelea chakula ambacho atakituma kana kwamba ni mkate. Waisraeli watakula hichi chakula kila siku, kama walivyo kula mkate kila siku kabla ya hichi.

Exodus 16:16

Sentensi Unganishi

Musa anaendelea kuwaambia watu kuhusu chakula Mungu anacho wapa.

lita

"lita mbili"

hawakuwa na kilicho salia

"hawakukosa chochote" au "walitosheka"

Exodus 16:22

siku ya sita

"siku ya 6"

mkate

Hii ya husu mkate uliyo tokea kama barafu kwenye ardhi kila asubui.

kujiliwaza

"umakini" au "tulivu na kuwaza"

Exodus 16:24

Haikuharibika

"haikunuka vibaya"

leo ni siku iliyo tengwa ya kumtukuza Yahweh

"leo ni Sabato na itumike tu kwa kumtukuza Yahweh.

Exodus 16:26

lakini siku ya saba

lakini katika siku ya saba"

manna

Hili lilikuwa jina Waisraeli walilipa mkate Yahweh aliyo usababisha utokea kila asubui.

hawakukuta

"hawakukuta mana yeyote"

Exodus 16:28

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaongea na Musa, lakini neno "wewe" la husu watu wote wa Israeli.

Kwa muda gani utaendelea kukataa kushika amri zangu na sheria zangu?

Mungu anatumia hili swali kuwa kemea watu maana hawakutii sheria zake.

kushika amri zangu na sheria zangu

"kutii amri zangu na sheria zangu"

Yahweh amekupa Sabato

Yahweh anaongea kuhusu kufundisha watu kupumzika Sabato kana kwamba Sabato ni zawadi.

siku ya sita ... siku mbili ... siku ya saba

"siku ya 6 ... siku 2 ... siku ya 7"

mkate

Hii ya husu mkate uliyo tokea kama barafu kwenye ardhi kila asubui.

Exodus 16:31

manna

Hili likuwa jina Waisraeli walilo lipa mkate ambao Yahweh alisababisha kutokea kila asubui.

mbegu ya mgiligani

Watu wanakausha mbegu na kusaga katika unga na kuweka kwenye chakula kuleta ladha.

maandazi

membamba kama biskuti

lita

"lita mbili"

mkate

Hii ya husu mkate uliyo tokea kama barafu kwenye ardhi kila asubui.

Exodus 16:33

Lita mbili ni makumi ya efa

Hivi ni vyombo vya vipimo. Wasomi wa kwanza waliweza jua kiasi gani efa ilikuwa. Hii sentensi ya weza saidia kujua kiasi gani lita ilikuwa.

lita

"lita mbili"

Exodus 17

Exodus 17:1

nyikani ya Sinu

Neno "Sinu" hapa ni jina la Kiebrania la nyikani. Sio neno la kiengereza lenye maana ya "dhambi"

Refidimu

Hii ina maana ya "sehemu ya kupumzika" sehemu ya kupumzika katika safari ndefu nyikani.

Kwanini mnagombana na mimi? Kwanini mnajaribu Yahweh?

Musa anatumia haya maneno kukemea watu.

Ili utuue sisi na watoto wetu na mifugo yetu kwa kiu?

Watu wanatumia hili swali kumshitaki Musa kwa kutaka kuwaua.

Exodus 17:4

Massa

"sehemu katika jangwa ambalo jina lake la maanisha "jaribu"

Meriba

"sehemu katika jangwa ambalo jina lake la maanisha "lalamika"

Exodus 17:8

Refidimu

Hii ilikuwa sehemu jangwani.

Hivyo Yoshua akapigana na Ameleki

Yoshua ana wakilisha Waisraeli aliyo waongoza kwenye pambano.

Huri

Huri alikuwa rafiki wa Musa na Aruni.

Exodus 17:11

Israeli ilikuwa yashinda ... Ameleki alianza kushinda

Maneno "Israeli" na "Ameleki" wana wakilisha wapiganaji kutoka hizo sehemu.

Mikono ya Musa alipo kuwa mizito

Mwandishi ana andika mikono ya Musa kuchoka kana kwamba mikono yake imekuwa mizito.

kwa upanga

Upanga wawakilisha pambano.

Exodus 17:14

nitaondoa kumbukumbu ya Ameleki

Mungu anaongea kuharibu Ameleki kana kwamba anaondoa kumbukumbu ya watu kuhusu Ameleki. Wakati kundi la watu linapo haribiwa, hakuna cha kuwakumbusha watu kuhusu wao.

mkono ulinyanyuliwa juu

Watu waliinua mkono wao wakati walipo weka ahadi au deni.

mkono ulinyanyuliwa juu

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Ameleki

Hii ya husu Waameleki.

Exodus 18

Exodus 18:1

baba mkwe wake Musa

Hii ya husu baba wa mke wa Musa.

akamchukuwa Zipora, mke wa Musa ... na wana wake wawili

Maana zinazo wezekana ni 1) Yethro alimchukuwa Zipora na wana wake wawili kwa Musa, au 2) Yethro alimkaribisha awali Zipora na wana wake wawili.

baada ya kumpeleka nyumbani

Hichi ni kitu Musa alicho fanya hapo awali. Maana yote yaweza fanywa wazi.

Gershomu

Huyu ni mwana wa Musa na Zipora, ambaye jina lake lina maana ya "mgeni"

Eliezeri

Huyu ni mwana wa Musa na Zipora ambaye jina lake lina maana ya "Mungu ndiye anaye ni saidia"

Exodus 18:5

alipo eka kambi

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 18:7

akamwinamia, na kumbusu

Haya matendo ya ishara yalikuwa namna ya kawaida watu walionyesha heshima kubwa na upendo katika huo utamaduni

kwa ajili ya Waisraeli

Neno "Israeli" la wakilisha watu wa Israeli.

magumu yote yaliyo watokea

Musa ana andika magumu kuwa tokea kana kwamba magumu yamewatokea.

Exodus 18:9

mkono wa Wamisri ... mkono wa Farao

Mkono una maana ya nguvu ya mtu kufanya kitu.

Exodus 18:13

Ni nini unachofanya na watu?

Yethro anatumia hili swali kumuonyesha Musa kwamba alicho kuwa anafanya si sawa?

Kwanini unaketi peke yako ... asubui hadi jioni?

Yethro anatumia swali kumuonyesha Musa alikuwa anafanya sana.

unaketi peke yako

Neno "keti" hapa ni mbadala wa "hukumu" Waamuzi walikuwa wana keti wanapo sikiliza malalamishi ya watu.

Exodus 18:17

Hakika utajichosha

"utajifanya kuchoka sana"

Huu mzigo ni mzito sana kwako

Yethro anazungumzia kazi ngumu Musa anayo fanya kana kwamba ni kazi ya mwili Musa alikuwa anabeba.

ushauri

"mwongozo" au "maelekezo"

Mungu ata kuwa na wew

Yethro anaongelea Mungu kumsaidia Musa kana kwamba Mungu ata kuwa na Musa.

leta malumbano yao kwake

Yethro anaongelea Musa kumwambia Mungu kuhusu malumbano kana kwamba Musa ana leta malumbano yao kwa Mungu.

Lazima uwafundishe njia yakutembea

Yethro anaongelea kuishi au kutenda kama kutembea.

Exodus 18:21

Sentensi Unganishi

Yethro anaendelea kuongea na Musa.

Mbali zaidi, lazima uchague

"kwa niongeza, lazima uchague"

maelfu, mamia, hamsini, na makumi

"makundi ya 1,000, makundi ya 100, makundi ya 50, na makundi ya 10"

Lazima uwaeke juu ya watu

Yethro anaongelea kuwapa mamlaka juu ya watu kama kuwaweka juu ya watu.

kesi za kawaida

"kesi rahisi"

kesi ngumu wataleta kwako

Yethro anaongelea kumwambia Musa kuhusu kesi ngumu kama kumletea kesi ngumu.

watabeba mzigo na wewe

Yethro anaongelea kazi ngumu ambayo watafanya kana kwamba ni mzigo watao beba.

kuvumilia

kila watakaacho vumilia cha weza wekwa wazi.

Exodus 18:24

vichwa juu ya watu

Musa ana andika viongozi wa watu kana kwamba ni kichwa cha mwili.

wanaume wenye uwezo

Kilicho kuwa wanaweza kufanywa cha weza andikwa wazi.

hali

"mazingira"

Kesi ngumu walimletea Musa

Mwandishi ana andika kumwambia Musa kuhusu kesi ngumu kama kumletea kesi ngumu.

kesi ndogo

"kesi zilizo rahisi"

Exodus 19

Exodus 19:1

Katika mwezi wa tatu ... siku hiyo

Hii ina maana walifika nyikani siku ya kwanza ya mwezi kama walivyo ondoka Misri siku ya kwanza ya mwezi. Siku ya kwanza ya mwezi wa tatu kwenye kalenda ya Kiebrania ni karibu na katikati ya Mei katika kalenda za Magharibi.

kutoka

"waliondoka"

Refidimu

Hii ni sehemu kando ya nyikani ya Sinai ambapo watu wa Israeli walikuwa kambini.

Exodus 19:3

nyumba ya Yakobo

Neno "nyumba" hapa la wakilisha familia na uzao wa Yakobo.

nyumba ya Yakobo, watu wa Israeli

Neno "watu wa Israeli" ina eleza nini "nyumba ya Yakobo" ina maanisha.

Uliona

Neno "Uliona" hapa linawakilisha Waisraeli. Yahweh anamwambia Musa nini cha kuwaambia Waisraeli.

nilivyo kubeba kwa mabawa ya tai

Mungu anaongelea kujali watu wake wakati walipo safiri kana kwamba yeye alikuwa tai na kuwabeba kwa mabawa yake.

ukinisikiliza kwa utii

Utii yaweza andikwa kama kitenzi.

sauti yangu

Sauti ya Munguya wakilisha anachosema.

kushika agano langu

"fanya kile agano langu linataka mfanye"

mali yangu ya pekee

"hazina"

ufalme wa kikuhani

Mungu anaongelea watu wake kana kwamba ni makuhani.

Exodus 19:7

Aliweke mbele yao maneno yote

Mwandishi ana andika kuhusu Musa kuwaambia watu vitu kana kwamba alikuwa ana weka maneno mbele yao.

maneno yote haya Yahweh aliyo muamuru

Neno "maneno" ya husu kile Yahweh alicho sema.

musa akaja kutoa taarifa

Pale Musa alipo enda pa weza andikwa wazi.

maneno ya watu

Neno "maneno" ya husu kile watu walicho sema.

Exodus 19:10

lazima uwatenge

Hii inaweza kuwa "waambie wajitoe kwangu" au "waambie wajitakase"

mavazi

"nguo"

Kuwa tayari

Hili lilikuwa amri kwa watu wa Israeli.

Exodus 19:12

Maeleo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuzungumza na Musa

Yeyote atakaye shika mlima ata uawa

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Yeyote atakaye shika

"Mtu yeyote atakaye gusa"

mtu huyu

"ambaye atafanya hivi"

lazima apigwe mawe au kuchomwa mshale

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

kuchomwa

Hii ya husu kufa kwa mtu anaye piga mishale kutoka kwenye upinde au jiwe kwenye manati.

Exodus 19:14

msiwakaribie wake zenu

Hii ni njia ya kistarabu ya kusema usilale na mke wako.

Exodus 19:16

waliogopa

"walitetemeka kwa hofu"

alishuka

"teremka chini"

kama moshi wa tanuru

Hii yaonyesha ni moshi mkubwa sana ulikuwa.

tanuru

shimo linalo weza fanywa kali sana kwa moto

Exodus 19:19

ongezeka na zaidi

"ikaendelea kuwa kubwa na kubwa"

kwa sauti

Neno "sauti" hapa ya husu sauti Mungu aliyo fanya. Maana inayo wezekana ni 1) kwa kuongea kwangu kama radi" au 2) "kwa kuongea" au 3) "kusababisha radi iongee"

akamuita Musa

"alimuita Musa kuja juu"

wasipite

Mungu aliongea kuhusu kupita mipaka kana kwamba wataweza vunja kizuio na kupita.

Exodus 19:23

shuka chini

"nenda chini"

kupita vizuizi

Mungu aliongea kuhusu kupita mipaka kana kwamba wataweza vunja kizuio na kupita.

Exodus 20

Exodus 20:1

nyumba ya utumwa

"sehemu mlliyo kuwa watumwa"

Msiwe na miungu mingine ila mimi tu

"Msiabudu miungu mingine zaidi yangu"

Exodus 20:4

kufananisha

"na usitengeneze cha kufanana"

wivu

Mungu anataka watu wake wamuabudu yeye tu.

Nitaadhibu uovu wa mabubu kwa kuleta adhabu juu ya kizazi

Mungu ata hadhibu watu kwa dhambi za wazazi wao

cha tatu hadi kizazi cha nne

"kizazi ch 3 na cha 4"

agano la uaminifu kwa maelfu

"kwasababu ya agano langu, ni mwaminifu kwa maelfu" au "napenda maelfu kwa uaminifu"

kwa maelfu watakao

"vizazi vingi vya hao"

Exodus 20:7

Usilitaje bure jina

"kutumia jina langu"

bure

"bila kujali" au "bila heshimu"

Exodus 20:8

ufanye kazi zako

"fanye kazi za kila siku"

malango yako

Miji mara nyingi ilikuwa na ukuta ikizunguka kuweka mbali maadui, na milango watu kuingia na kutoka.

siku ya saba

Hapa "saba" ni namba "7"

aliibariki siku ya Sabato

Maana zinazo wezekana ni 1) Mungu alisababisha Sababto kuzalisha matokea mazuri, au 2) Mungu alisema siku ya Sabato ni nzuri.

kuitenga

"kuitenga kwa kusudi maalumu"

Exodus 20:12

Usifanye uasherati

"usifanye ngono na mtu yeyote zaidi ya mpenzi wako"

Exodus 20:15

Usishuhudie uongo

"usiongea taarifa ya uongo"

Usitamani

"usitamani kuwa nacho sana" au "usitake kuchukuwa"

Exodus 20:18

mlima ukitoa moshi

"moshi ukitoka mlimani"

walitetemeka

"walitetemeka kwa hofu"

walisimama mbali

"walisimama kando"

ili heshima yake iwe ndani yenu, kwa hiyo msitende dhambi

"ili mumheshimu yeye na msitende dhambi"

alikaribia

"alisogea karibu na"

Exodus 20:22

Ni lazima uwaambie hili Waisraeli

"Waambie Waisraeli hili"

Wewe mwenyewe umeona niliongea na wewe kutoka mbinguni

"Umesikia nikiongea na wewe kutoka mbinguni"

Misjitengenezee miungu mingine pamoja nami

"Usifanye sanamu kama miungu mingine zaidi yangu"

miungu ya fedha au miungu ya dhahabu

"miungu iliyo tengenezwa kwa fedha au dhahabu"

Exodus 20:24

madhabahu ya udongo

madhabahu iliyo tengenezwa kwa vitu vya ardhini, kama mawe, mchanga, au udogo

ntakapotaka jina langu liheshimiwe

Hapa "jina" linasimama kwa niaba ya utu wa Mungu.

msije juu ya madhabahu yangu kwa hatua zenu

"Msitengeneze madhabahu yenye ngazi"

msioneshe sehemu zenu za siri

"kuonyesha mwili wenu wa uchi"

Exodus 21

Exodus 21:1

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa

utakazoweka kabla yao

"lazima uwape" au "utawaambia"

Exodus 21:2

Maelezo ya Jumla

Yahweh anamwambia Musa sheria zake kwa watu wa Israeli.

Kama alikuja mwenyewe, ataenda huru kwa ridhaa yake

"Mwenyewe" inaweza andikwa wazi.

mwenyewe

"pekee yake" au "bila mke"

Exodus 21:5

atasema waziwazi

"kusema wazi"

sitaenda nje huru

"sitaki bwana wangu aniachie huru"

atatoboe sikio lake

"kuweka tobo sikioni"

sindano

kipini kinacho tumika kueka shimo

maisha yake yote

"mpaka mwisho wa maisha yake'

Exodus 21:7

aliye mtenga

"aliye chague"

lazima amnunue tena

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Hana ruhusa ya kumuuza

"hana mamlaka ya kumuuza"

amemtendea kwa hila

"kamadanganya"

Exodus 21:9

aliyetenga

"chagua"

apaswi kupunguza chakula chake, mavazi, au haki za ndoa

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

punguza

"kuchukuwa"

haki za ndoa

Hii ina husisha vitu mme wake anapaswa kufanya kwa ajili ya mke wake, pamoja na kulala naye.

Exodus 21:12

piga

"shambulia"

huyo mtu lazima auwawe

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

kufanya pasipo kukusudia

"hakupanga kufanya" au "hakufanya kwa kusudia"

nitaanda sehemu ya yeye kukimbilia

Kusudi la kuchagua sehemu laweza andikwa wazi hapa.

kwa kadiri ya mbinu erevu

"baada ya kufikiria kwa uangalifu"

Hili afe

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 21:15

Yeyote atakaye mpiga baba au mama yake lazima auawe

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

lazima

"hakika"

mali yake

"pamoja naye"

huyo mtekaji lazima auawe

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

eyote atakaye mlaani baba au mama yake lazima auawe

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 21:18

alazwe kitandani

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

akapona

"akapata nafuu"

gongo

Hii ni fimbo inayo weza egemewa wakati wakutembea.

muda aliye mpotezea

Hii ya husu hali wakati mtu hawezi pata pesa.

alipe matibabu yake yote

"gharama za matibabu"

Exodus 21:20

kwa madhara ya pigo

"kwasababu ya majeraha"

huyo mtu lazima ahadhibiwe

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

kwa kuwa atateseka kupoteza mtumishi huy

Waweza eleza wazi katika tafsiri mtumishi alikuwa na dhamani kwa bwana wake.

Exodus 21:22

mimba na kuiharibu

"mtoto akafa tumboni mwake"

mwanaume mwenye hatia lazima alipe

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

kama hakimu anavyo kusudia

"alicho amuua muamuzi"

lazima utoe uhai kwa uhai, jicho kwa jicho

Hii ina maana kama kaumia, mtu aliye muumiza lazima aumizwe vivyo hivyo.

Exodus 21:26

Kama mwanaume

Hapa "mwanaume" ya husu mmiliki wa mtumwa.

fidia

Fidia ni kitu mtu anafanya kwa mtu mwingine au anampa mtu mwingine kwa kile alicho sababisha kupoteza.

Exodus 21:28

ng'ombe lazima apigwe mawe

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

nyama yake hairuhusiwi kuliwa

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

mmiliki wa ng'ombe lazima awe huru

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

mmiliki wake lazima auawe pia

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Kama malipo ya uhai yanaitajika

Kama mmiliki wa ng'ombe anaweza kulipa gharama ya kuokoa maisha yake, kisha anapaswa kulipa chochote waamuzi wanachotaka.

Exodus 21:31

ng'ombe amempiga

"kajeruhi kwa pembe zake"

shekeli thelathini za fedha

"gramu 330 za fedha"

ng'ombe lazima apigwe mawe

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 21:33

akifungua shimo

"funua shimo kwenye ardhi"

alipe madhara

Mmiliki lazima alipe kwa madhara ya mnyama.

atakuwa wake

Aliye lipa madhara ya mnyama atakuwa mmliki wa mnyama aliye kufa na anaweza fanya ancho taka.

Exodus 21:35

kugawana gharama

"gawanya pesa"

kama ilijulikana

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

tabia ya kupiga hapo awali

"kapiga wanyama wengine kabla"

mmiliki wake hakumfunga ndani

Hii ina maana mmiliki hakumhifadhi ng'ombe kwa usalama ndani ya uzio.

lazima alipe ng'ombe kwa ng'ombe

Mmiliki wa ng'ombe aliye ua lazima atoe ng'ombe kwa aliye poteza ng'ombe wake.

Exodus 22

Exodus 22:1

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa sheria zake kwa ajili ya watu wa Israeli.

Kama mwizi akikutwa

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

anavunja ndani

"akitumia nguvu kuingia ndani ya nyumba"

kama akipigwa na kufa

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

hakutakuwa na hatia ya mauaji hayatakuwa juu ya mtu yeyote

"hakuna atakaye kuwa na hatia ya kumuua"

kama jua limechomoza kabla ya yeye kuvunja ndani

"kama kuna mwanga kabla hajaingia"

hatia ya mauaji itakuwa juu ya aliyemuua.

"huyo mtu atakaye muua akatakuwa na hatia ya mauaji"

lazima auzwe kwa uwizi wake

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Kama mnyama amekutwa hai eneo lake

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 22:5

Kama mwanaume akiwapeleka malishoni mifugo yake

"kama mwanaume akimuacha mnyama wake kulala mimea"

malishoni

"inapo kula mimea"

lazima afanye malipo

Lazima amlipe mmiliki wa hilo shamba"

Exodus 22:6

Kama moto ukitokea na kusambaa kwenye miba

"Kama mtu akianza moto na kusambaa kwenye miba"

kusambaa kwenye miba

"kupita kwenye mimea iliyo kauka"

shamba kuteketezwa

"moto kuteketeza shamba"

lazima afanye malipo

"lazima alipe mbegu moto ulizo haribu"

Exodus 22:7

amtunzie

"kuangaliza" au "kuweka salama"

kama itaibiwa

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

mwizi

mtu anaye iba

kama mwizi akipatikana

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

kuja mbele za waamuzi

"kuja mbele za waamuzi ili waweze jua kama"

ameeka mkono wake kwenye mali za jirani yake

Huu ni msemo. Kama namna ya kusema hivi katika lugha yako, waweza sema hapa.

malalamiko ya pande zote lazima zije kwa waamuzi

Waamuzi lazima wasikilize watu wote wawili wanao dai vitu ni vyao na waamuzi wataamua nani ana hatia.

Exodus 22:10

kiapo kwa Yahweh lazima wafanye wote wawili

Mtu aliye shutumiwa kuiba mnyama lazima aape kiapo. Mmiliki wa mnyama aliye potea lazima akubali kiapo kilicho apiwa.

Lakini kama iliibwa kwake

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Kama mnyama alikatwa vipande

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Hatalipa kwa ajili ya vile vipande

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 22:14

lazima afanya malipo

"lazima alipe kwa mnyama mwingine"

kama mnyama aliazimwa

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

atalipwa kwa gharama ya kuazima

Aliye azima mnyama hata mlipa mmiliki zaidi ya ada au gharama ya kukodisha. Hii ada italipa kwa nyama aliye potea.

gharama ya kuazima

"ada ya kukodisha" au "pesa iliyo lipwa kukodisha mnyama"

Exodus 22:16

akimtongoza

"kushawishi"

hana mchumba

"haja ahidiwa kuolewa"

akilala naye

Kulala na mtu ni tafsida ya kufanya ngono.

gharama za bibi arusi

"mahari"

Exodus 22:18

Yeyote atakaye lala na mnyama lazima auawe

Hapa "lala na mnyama" ni tafsida yenye maana ya kufanya ngono na mnyama.

Exodus 22:20

Yahweh lazima auawe

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

mkosea mgeni

"kutendea vibaya mgeni"

Exodus 22:22

Hauruhusiwi kumtendea vibaya mjane au mtoto asiye kuwa na baba

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

mjane

"mwanamke aliye poteza mme wake"

mtoto asiye kuwa na baba

"yatima"

nitakuua kwa upanga

Kuuawa "kwa upanga" ni mbadala yenye maana mtu atakufa vibaya sana.

Exodus 22:25

kutoza faida

"kulipisha kwa pesa ya faida kwa kuazima"

funiko lake

"koti pekee"

Nini tena ambacho anaweza kulalia?

Hili swali latilia msisitizo.

mwenye huruma

"rehema" au "neema"

Exodus 22:28

Husinikufuru mimi, Mungu

"Husimtukane Mungu"

wala kumtukana mtawala

"na usimuombe Mungu kufanya kitu kibaya kwa mtawala"

Exodus 22:29

Husizuie sadaka

Hii yaweza andikwa katika tensi chanya.

unipe mzaliwa wa kwanza wa wana wako

"waweke wakfu wazaliwa wenu wa kwanza kwangu"

ufanye hivyo hivyo kwa

"niwekee wakfu wazaliwa wa kwanza wa"

Kwa siku saba

Hii yaweza andikwa kama namba

siku ya nane

Hii yaweza andikwa kama namba.

unipe mimi

"waweke wakfu kwangu"

Exodus 23

Exodus 23:1

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumuambia Musa sheria zake kwa watu wa Israeli.

taarifa ya uongo

Hii ni sawa na kudanganya au shuhuda ya uongo

wala kutoa ushahidi

"na wewe husizungumze"

ukiwa na umati

Hili ni fumbo linalo eleza mtu kukubaliana na kundi la watu kana kwamba alienda na kusimama na hilo kundi.

kupotosha haki

fanya yasio halali au matendo yasio ya kijamii yenye matokeo ya uwamuzi usio haki

Exodus 23:4

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa sheria zake kwa watu wa Israeli.

Exodus 23:6

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa sheria zake kwa watu wa Israeli.

Haupaswi kupotosha haki

"Husifanye matendo yanayo zalisha matokea yasio halali" ambayo uleta uhuru kwa mwenye hatia au hukumu kwa hasiye na hatia.

sitamuacha muovu

"sitampata muovu bila hatia"

rushwa inawapofusha ... kupotosha

Hapa "rushwa" inaelezwa kama ni mtu.

Exodus 23:10

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa sheria zake kwa watu wa Israeli.

mazao

"chakula kutoka kwenye mimea"

hakujalimwa

"hakujapaliliwa"

ili kwamba maskini miongoni mwenu wale

Maskini wale chakula chochote kinacho ota chenyewe shamba lisilo paliliwa.

Exodus 23:12

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa sheria zake kwa watu wa Israeli.

Kuwa makini kwa

"fanya" au "tii"

ng'ombe na punda wako

"wanyama wa kazi zako"

wageni wapumzike na kupata hauweni

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Husitaje majina ya miungu mingine

Hapa "majina" ni mbadala wa kuomba kwa miungu mingine.

Exodus 23:14

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa sheria zake kwa watu wa Israeli.

Abibu

Hili ni jina la mwezi wa kwanza wa kalenda ya Kiebrania. Abibu ni wakati wa sehemu ya mwisho ya Machi na sehemu ya kwanza ya Aprili kwa kalenda za Magharibi.

Exodus 23:16

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa sheria zake kwa watu wa Israeli.

Lazima uadhimishe

"Lazima uheshimu"

Sherehe ya Ukusanyaji

Hii sherehe ya sherekewa mwishoni mwa mavuno ya mazao ya mwaka.

Wanaume wote wako lazima wajitokeze

Hapa "kujitokeza" kuna maana ya kukusanyika kwa ibada.

Exodus 23:18

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa sheria zake kwa watu wa Israeli.

Mafuta kutoka kwa dhabihu

Mafuta yalichomwa kama sadaka kwa Yahweh na hayakuliwa.

matunda ya kwanza bora

"bora na mazao ya kwanza ya mavuno"

Haupaswi kumchemsha mbuzi mtoto akiwa bado ananyonya

Hii ilikuwa zoezi la kishirikina miongoni mwa Wakanani, ambalo Waisraeli hawakuruhusiwa kushiriki.

Exodus 23:20

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa sheria zake kwa watu wa Israeli.

Kuwa makini naye

"Msikilize"

Husimkasirishe, kwa kuwa hatasamehe

"hukimkasirisha, hatasamehe"

Jina langu liko kwake

Hapa "jina" la husu mamlaka ya Mungu.

hakika ukimtii sauti yake

Hapa "sauti" ya wakilisha kile malaika anasema.

adui kwa adui zako na mpinzani kwa wapinzani wako

Hii mistari miwili ina maana ya kitu kimoja na yana tumika kuweka mkazo.

Exodus 23:23

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa sheria zake kwa watu wa Israeli.

Haupaswi ... kufanya wanavyo fanya

Waisraeli hawapaswi kuishi kama watu wanao muabudu Mungu mwingine.

Exodus 23:26

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa sheria zake kwa watu wa Israeli.

Hakuna mwanamke atakaye kuwa tasa au mimba kuharibika katika nchi yako

Hii yaweza andikwa katika tensi chanya.

mimba kuharibika

mimba kufika mwisho mapema na pasipo tarajia

mavu

mdudu anaye paa na anaweza uma watu na kusababisha maumivu

au nchi itakuwa imetelekezwa

"kwasababu hakuna atakaye kuwa anaishi nchini"

Exodus 23:30

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa sheria zake kwa ajili ya watu wa Israeli.

hakika watakuwa mtego kwako

Hii ina maana ya kuabudu miungu mingine itawapeleka watu wa Israeli kwa uharibifu.

Exodus 24

Exodus 24:1

Nadabu ... Abihu

Haya ni majina ya wanaume.

wazee sabini wa Israeli

"wazee 70 wa Israeli"

Exodus 24:3

kwa sauti moja

Huu ni msemok wenye maana watu walikubaliana.

mguu wa mlima

"tako la mlima"

Exodus 24:5

Musa allichukuwa nusu ya damu na kuweka kwenye mabeseni

Musa alikusanya nusu ya damu kwenye mabesini ili kuwanyunyuzia watu 24:7. Hii itawathibitishia watu ushiriki wao katika agano kati ya watu wa Israeli na Mungu.

alinyunyuzia nusu ingine kwenye madhabahu

Hapa madhabahu ya wakilisha Mungu. Hii itathibitisha ushiriki wa kati ya Mungu na watu wa Israeli.

Exodus 24:7

Tutakuwa watiifu

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Kisha Musa akachukuwa damu

Hii ya husu damu ambayo Musa aliweka kwenye bakuli.

Exodus 24:9

Nadabu ... Abihu

Haya ni majina ya wanaume.

Chini ya miguu

Hii ina muongelea Mungu kana kwamba alikuwa na miguu ya mwanadamu.

sakafu iliyo jengwa kwa jiwe la yakuti samawi

"sakafu iliyo tengenezwa kwa mawe ya buluu yanayo itwa yakuti samawi"

sakafu

ardhi ngumu iliyo tengenezwa kwa kutembelea au kuendeshea

jiwe la yakuti samawi

Hii ni dini ambalo ni buluu kwa rangi.

safi kama mbingu yenyewe

Hili ni fumbo.

Mungu hakugusa na mkono kwa hasira viongozi Waisraeli

Hii ina maana kuwa Mungu hakujeruhi viongozi.

Exodus 24:12

saani za mawe na sheria na amri

Mungu aliandika sheria na amri katika saani za mawe.

na msaidizi wake Yoshua

"na Yoshua aliye msaidia"

Exodus 24:14

mtusubiri

"msubiri Yoshua na mimi"

Huri

Huri alikuwa mwanaume aliye kuwa rafiki wa Musa na Aruni.

Exodus 24:16

Utukufu wa Yahweh

Huu ulikuwa mwanga mzuri wa uwepo wa Mungu.

kama moto ulao

Hii ina maana ya utukufu wa Yahweh ulikuwa mkubwa una ulionekana kuwaka kwa mwanga kama moto.

kwenye macho ya Waisraeli

Hapa "macho" ya husu mawazo ya kuhusu walicho kiona

siku arobaini na usiku arobaini

"siku 40 na usiku 40"

Exodus 25

Exodus 25:1

atakayetoa kwa moyo mkunjufu

Huu ni msemo unao hashiria tamanio la mtu kutoa sadaka.

Lazima upokee

Neno "upokee" la husu Musa na viongozi.

Exodus 25:3

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa ni watu wafanye.

buluu, zambarau na nyekundu

Maana zinazo wezekana ni 1) "vitu iliyo tiwa buluu, zambarau, na nyekundu," 2) "buluu, zambarau na nyekundu" kupaka kitambaaa.

pomboo

mnyama mkubwa anaye ishi baharini na kula mimea

shohamu

jiwe la thamani lenye miisho meupe na meusi, nyekundu au kijivu.

mawe mengine ya kutiwa

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 25:8

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa ni watu wafanye.

patakatifum ... maskani

Haya maneno yana maana moja.

Lazima ufanye

Hapa "ufanye" ni wingi na ya husu Musa na watu wa Israeli.

nikuoneshayo mfano

"kukuonyesha katika mpango wake" au "nikuonyeshayo katika ramani"

Exodus 25:10

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

dhiraa mbili na nusu ... dhiraa moja na nusu

"dhiraa 2.5 ... dhiraa 1.5"

Exodus 25:12

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

viduara vinne vya dhahabu

Hii ilikuwa namna dhahabu ya yayushwa, ilikuwa ya miminwa katika chombo cha mviringo, kisha kuwachwa kuwa ngumu.

ili kulichukua hilo sanduku

"ili uweze kubeba sanduku"

Exodus 25:15

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

kifuniko cha dhahabu

Hichi ni kifuniko kinacho keti juu ya sanduku ambapo sadaka ya maombezi ufanyika.

dhiraa mbili na nusu ... dhiraa moja na nusu

"dhiraa 2.5 ... dhiraa 1.5"

Exodus 25:19

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

kifuniko cha dhahabu

Hichi ni kifuniko kinacho keti juu ya sanduku ambapo sadaka ya maombezi ufanyika.

Lazima uweke

Hapa "uweke" ya husu Musa na watu wa Israeli.

Exodus 25:22

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa.

nitaonana nawe hapo katika sanduku

"Nitakutana na wewe katika sanduku"

kifuniko cha dhahabu

Hichi ni kifuniko kinacho keti juu ya sanduku ambapo sadaka ya maombezi ufanyika.

Exodus 25:23

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

dhiraa mbili na nusu ... dhiraa moja na nusu

"dhiraa 2.5 ... dhiraa 1.5"

Exodus 25:25

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

fremu ya kuizunguka

"fremu ya meza"

ilipo kuwa

"ilipo"

kuichukulia

"ili kubeba"

Exodus 25:28

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

ile meza ichukuliwe kwayo

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

vya kumiminia

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

mikate ya wonyesho

Huu mkate uliwakilisha uwepo wa Mungu.

Exodus 25:31

dhahabu safi

"dhahabu iliyo gongwa"

kinara na kifanywe

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

kitako chake, na mti wake, vikombe vyake, na matovu yake, na maua yake, vyote vitakuwa vya kitu kimoja nacho

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 25:33

Maelezo ya Jumla

Mungu anaendelea kumwambia Musa nini watu wafanye. Yahwe anaelezea kinara cha taa.

maua ya mlozi

nyeupe au maua ya pinki yenye majani matano

Exodus 25:35

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

kitu kimoja nacho

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 25:37

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

zitoe nuru mbele yake

"hivyo watoa mwangaa"

Na makoleo yake, na visahani vyake, vyote vitakuwa vya dhahabu safi

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

talanta moja

Talanta ina kilogramu 34

na vyombo

makoleo na visahani

uliooneshwa mlimani

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 26

Exodus 26:1

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

Lazima ufanye

Yahweh anaongea na Musa, hivyo neno "ufanye" la husu yeye. Yahweh inawezekana alitarajia Musa kumwambia mtu mwingine kufanya kazi, lakini Musa atakuwa ana wajibika kuona kuwa kazi imefanywa sahihi.

mapazia

Haya yalikuwa vitambaa vikubwa vya kushona vilivyo tumika kutengeneza kifuniko na kuta za kugawanya patakatifu.

dhiraa ishirini na nane ... dhiraa nne

"dhiraa 28 ... dhiraa 4." Dhiraa ni sentimita 46.

Mapazia matano yataungwa pamoja ... yataungwa pamoja

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 26:4

tanzi ... vifungo

Vifungo vinatoshea kwenye tanzi ili kushikilia pazia pamoja.

fungu

"fungu moja la mapazia matano"

fungu la pili

"fungu la pili la mapazia matano"

Exodus 26:7

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

kumi na moja ... thelethini ... nne

"11 ... 30 ... 4"

dhiraa

Dhiraa ni sentimita 46

Exodus 26:10

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

tanzi ... vifungo

Vifungo vinatoshea kwenye tanzi ili kushikilia pazia pamoja.

Exodus 26:12

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

dhiraa

Dhiraa ni sentimita 46

Exodus 26:15

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

fremu

Hii ya husu fremu walizo tengeneza kwa kuunganisha mbao ndogo vya vipande.

dhiraa kumi ... dhiraa moja na nusu

"dhiraa 10 ... dhiraa 1.5"

Exodus 26:19

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

vitako vya fedha

Hivi vilikuwa vitofali vya fedha vyenye mpangilio kuweza ustahimili.

Lazima kuwe na vitako viwili

Hii ina weza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 26:22

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

Hizi fremu zitakuwa zimetengana upande wa chini, lakini zimeshinkana kwa juu ya duara moja

Hii ya weza andika katika tensi tendaji.

vitako vya fedha

Haya yalikuwa matofali yenye mpangilio kuweka fremu sehemu yake.

Exodus 26:26

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

mataruma

Hizi ni nguzo zinazo weka imara jengo.

maskani ulio nyuma kuelekea magharibi

Mbele ya maskani ili elekea mashariki.

Exodus 26:29

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa jinsi maskani itengenezwe.

kuwa kama vishikizo

"vitakavyo shika mataruma"

mataruma

Hizi ni nguzo zinazo weka imara jengo.

uliooneshwa mlimani

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 26:31

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa jinsi maskani itengenezwe.

Nawe fanya

Yahweh anazungumza na Musa, hivyo neno "nawe" la muhusu yeye. Yahweh inawezekana alitarajia Musa kumwambia mtu mwingine kufanya kazi, lakini Musa atakuwa ana wajibika kuona kuwa kazi imefanywa sahihi.

vifungo

Vifungo vintoshea kwenye tanzi kushikilia pazia pamoja.

nawe lete lile sanduku la ushuhuda

Sanduku la agano ni chombo linalo hifadhi amri.

Lile pazia litawagawanyia kati ya patakatifu

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 26:34

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

juu ya lile sanduku la ushuhuda

"kwenye chombo chenye amri"

Lile meza utaiweka upande wa kaskazini.

Hii ni meza inayo shikilia mkate unao wakilisha uwepo wa Mungu.

Exodus 26:36

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa jinsi ya kutengeneza patakatifu.

kisitiri

Hili lilikuwa pazia kubwa lilo tengenezwa kwa kitambaa.

buluu, zambarau, na nyekundu

Maana zinazo wezekana ni 1) "vitu iliyo tiwa buluu, zambarau, na nyekundu," 2) "buluu, zambarau na nyekundu" kupaka kitambaaa.

kitani nzuri yenye kusokotwa

Hii ilikuwa kitambaa kilicho tengenezwa kutokana uzi ambao mtu alizokota pamoja kufanya uzi mgumu.

mshonaji

"mtu anaye shona michoro ya vitambaa"

Exodus 27

Exodus 27:1

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa nini watu wafanye.

urefu wake dhiraa tano na upana wake dhiraa tano

"mita 2.2 kila upande"

madhabahu itakuwa mraba na kwenda juu kwake kutakuwa dhiraa tatu

"madhabahu itakuwa mraba na mita 1.3 kwenda juu"

dhiraa

dhiraa ni sentimita 46

Nawe fanya pembe nne kama mfano wa pembe za ng'ombe

"Nawe fanya muonekano wake kama pembe za ng'ombe katika miisho yake"

pembe zitakuwa

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji

utayafunika

" lazima ifunike madhabahu na pembe"

Exodus 27:3

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa nini watu wafanye.

mabakuli

"mabeseni"

meko

Kulikuwa na meko iliyo shika makaa kutoka madhabahuni.

Vyombo

Haya yalikuwa vifaa au vitu vilivyo tumika kwa kusudi.

Nawe uifanyie hiyo madhabahu wavu wa shaba

"Nawe ufanye wavu wa shaba kwa ajili ya madhabahu"

Exodus 27:5

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa nini watu wafanye.

Nawe lazima uweke huo wavu chini ya kizingo kiizungukacho madhabahu

Wavu uliwekwa ndani ya madhabahu.

Nawe fanya miti kwa ajili ya madhabahu

Hii miti ilitumika kubeba madhabahu.

Exodus 27:7

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa nini watu wafanye.

Na hiyo miti itatiwa katika viduara, na ile miti itakuwa katika pande mbili za madhabahu, wakati wa kuichukua

Hii yaweza andikwa katika sentensi tendaji.

ulivyooneshwa mlimani

Hii yaweza andikwa katika sentensi tendaji.

Exodus 27:9

kutakuwa na chandarua ya nguo

Hii yaweza andikwa katika sentensi tendaji.

chandarua ya nguo ya kitani nzuri yenye kusokotwa

chandarua ilikuwa pazia kubwa lilio tengenezwa na kitambaa

kitani nzuri yenye kusokotwa

Hichi kilikuwa kitambaa kutokana na nyuzi mtu alizo zokota pamoja kufanya uzi mgumu.

dhiraa mia moja

"mita 44"

nguzo

kipande kigumu cha mbao kilicho nyooshwa na kutumika kushikilia

Exodus 27:11

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa nini watu wafanye.

hiyo chandarua utakuwa

Hii yaweza andikwa kama amri.

nguzo zake kumi

Hii yaweza andikwa kama amri.

Na upana wa ule ua upande wa mashariki kuelekea mashariki utakuwa ni dhiraa hamsini

Hii yaweza andikwa kama amri.

Exodus 27:14

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa nini watu wafanye.

Chandarua

Hii ilikuwa pazia lililo tengenezwa kwa kitambaa.

nguzo

Hizi zilikuwa vipande vigumu vya mbao vilivyo nyooshwa juu.

vitako

Hizi zilikuwa matofali ya chuma yenye nafasi ya kushikilia nguzo

dhiraa kumi na tano

kiasi cha mita saba

Na kwa lile lango la ua patakuwa na kisitiri cha dhiraa ishirini

Hii yaweza andikwa kama amri.

kitakuwa cha nguo ... kitani nzuri yenye kusokotwa, kazi ya mshonaji

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

buluu, zambarau na nyekundu, na kitani nzuri yenye kusokotwa

Maana inayo wezekana ni 1) "kitambaa kilicho tiwa buluu, zambarau, na nyekundu," 2) "buluu, zambarau, na nyekundu"

mshonaji

mtu anaye shona mishono kwenye nguo

Exodus 27:17

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa nini watu wafanye.

dhiraa mia moja

"dhiraa 100"

yawe ya nguo ya kitani nzuri

Hii ilikuwa nguo iliyo tengenezwa kwa nyuzi mtu aliye sokota kufanya uzi mgumu.

Vyombo vyote vya maskani vitumiwavyo katika utumishi wake wote, na vigingi vyake vyote, na vigingi vyote vya ule ua, vitakuwa vya shaba

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 27:20

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa nini watu wafanye.

hema ya kukutania

Hili ni jina lingine la maskani.

itakuwa ni amri ya milele

"nianataka watu wafanye hii kama amri ya kudumu"

Exodus 28

Exodus 28:1

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

Umuite

Neno "Umuite" lina husu Musa.

Nadabu, na Abihu, na Eleazari, na Ithamar

Haya ni majina ya wanaume.

Nawe utamfanyia

Hapa "Nawe" ya husu watu.

Exodus 28:4

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

kanzu ya kazi ya urembo

"kanzu iliyo shoneshewa urembo"

kilemba

kitambaa kirefu cha kichwa kinacho zungushwa kichwani mara kadhaa.

mshipi

kipande cha kitambaa watu wanacho vaa kwenye kiuno au kwenye kifua

Exodus 28:6

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

kitani nzuri yenye kusokotwa

Hii ilikuwa nguo iliyo tengenezwa kwa nyuzi mtu aliyo sokotwa pamoja kufanya uzi mgumu.

kazi ya mstadi

mtu anaye weza kufanya vitu vizuri kwa mkono

ya vitu vile vile

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

shohamu

Haya ni mawe yenye miisho meupe na meusi, nyekundu au kahawia.

Exodus 28:10

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

Kwa kazi mtu mwenye kuchora mawe kama vile muhuri ichorwavyo

"Jinsi mtu anavyo chora kwenye muhuri"

mtu mwenye kuchora

mtu anaye kata michoro kwenye vitu vigumu kama mbao, jiwe, au chuma

vijalizo

vipande vya chuma vinavyo shikilia jiwe kwenye naivera

Exodus 28:13

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

vijalizo

vipande vya chuma vinavyo shikilia jiwe kwenye naivera

mikufu miwili ya dhahabu safi; utaifanya iwe mfano wa kamba

"mikufu miwili ya dhahabu yenye kusokotwa kama kamba"

Exodus 28:15

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

kazi ya fundi stadi; utakifanya kwa kuiandama ile kazi ya hiyo naivera

"fundi stadi atafanya kama ile naivera"

shibiri

Shibiri ni sentimita 22.

Exodus 28:17

vito

"madini ya dhamani" au "madini ya hazina"

akiki ... yaspi

Haya ni madini ya thamani.

yakuti

Hili ni jiwe la dini lenye rangi ya buluu

shohamu

Hili ni jiwe la thamani lenye miisho meupe na meusi, nyukundu au kahawia.

Vito hivyo vitakazwa ndani ya dhahabu kwa kujaa mahali pake

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 28:21

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

Na vile vito vitakuwa sawasawa

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

mfano wa kamba, ya kazi ya kusokotwa, ya dhahabu safi

"mikufu iliyo fanywa kwa dhahabu safi na imesokotwa kama kamba"

Exodus 28:25

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

mikufu miwili ya kusokotwa

"mikufu iliyo sokotwa kama kamba"

vile vijalizo viwili

Hizi ni vijalizo viwili vinavyo funga mawe.

Exodus 28:27

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

mshipi wa naivera uliosukwa kwa ustadi

Huu ulikuwa mkanda wa kitambaa uliyo tengenezwa kwa nyuzi nyembamba mtu alizo zokota kufanya uzi mgumu.

ili kwamba kikae

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

ili kwamba kifuko cha kifuani kisiachane na naivera

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 28:29

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

atayachukua majina ya wana wa Israeli katika kile kifuko cha kifuani

Hii ya husu majina ya makabila yaliyo chorwa katika mawe kumi na mbili.

cha kifuani

"katika moyo wa Aruni" au "kifuani mwake"

hizo Urimu na Thumimu ... atachukua hukumu ya

Huu mstari wapili unaeleza hizo Urimu na Thumimu na kusudi lake.

hizo Urimu na Thumimu

Haiko wazi hizi ni nini. Vilikuwa vitu, labda mawe, ambayo makuhani walitumia kufahamu mapenzi ya Mungu.

Exodus 28:31

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

Exodus 28:33

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

komamanga

Komamanga ni tunda la mviringo lenye ganda jekundu.

Kengele ya dhahabu na komamanga

Huu mstari umerudiwa kuonyesha ramani ya mchoro kwenye kanzu.

na sauti ya hizo kengele itasikilikana

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

ili kwamba asife

Ina hashiriwa kwamba ata kufa kwasababu hakumtii Yahweh.

Exodus 28:36

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wafanye.

kuchora juu yake, mfano wa machoro ya muhuri

"andika juu yake jinsi mtu anavyo chora kwenye muhuri"

kilemba

kitambaa kirefu cha kichwa kinacho zungushwa kichwani mara kadhaa.

Nalo litakuwa katika kipaji cha uso cha Aruni

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

alo litakuwa katika kipaji chake cha uso sikuzote

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 28:39

Maelezo ya Jumla

Mungu anaendelea kumwambia Musa nini watu wafanye.

kilemba

kitambaa kirefu cha kichwa kinacho zungushwa kichwani mara kadhaa.

mshipi

Mshipi ni kipande cha kitambaa ambacho mtu anavaa kwenye kiuno chake au kwenye kifua.

kazi ya mwenye kutia taraza

Mtia taraza ni mtu anaye shona michoro kwenye kitambaa.

Exodus 28:40

Maelezo ya Jumla

Mungu anaendelea kumwambia Musa nini watu wafanye.

mshipi

kipande cha kitambaa watu wanacho vaa kwenye kiuno au kwenye kifua

kofia

Kofia hii ni nyembamba, ya urembo ambayo mtu ni kitambaa mtu anacho vaa kichwani juu ya macho.

Nawe mvike huyo nduguye Aruni

Aruni alikuwa kaka mkubwa wa Musa.

Exodus 28:42

Maelezo ya Jumla

Mungu anaendelea kumwambia Musa nini watu wafanye.

suruali za nguo ya kitani

Hizi zilikuwa nguo za ndani, nguo zinazo valia njee ya nguo za njee, karibu na ngozi.

hema ya kukutania

Hili ni jina lingine la maskani.

amri ya milele

"sheria hisiyo kwisha"

Exodus 29

Exodus 29:1

Sasa

Neno "sasa" linaeka alama katika somo kutoka mavazi ya makuhani kwenda kutengwa kwa makuhani.

wapaswa kufanya

Hapa "wapaswa" ya husu Musa.

kuwatenga

"kumtenga Aruni na wana wake"

wanitumikie

Hii ya husu Yahweh.

mtoto wa ng'ombe dume

ng'ombe dume

Pia chukuwa maandazi bila hamira yalio pakwa mafuta

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

mkate ... keki ... maandazi

Hivi ni aina tofauti vya vyakula vya ngano.

Exodus 29:3

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa

Lazima uweke

"Lazima uweke mkate, keki, na maandazi"

na kuleta pamoja na ng'ombe dume na wana kondoo wawili

Hpa "kuleta" ina maana ya kutoa dhabihu. Maana kamili ya hii yaweza tafsiriwa kwa wazi.

hema la kukutania

Hili ni jina lingine la maskani.

Exodus 29:5

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa.

kanzu

Hili lilikuwa kanzu lilo shoneshewa mchoro.

mshipi wa naivera uliosukwa kwa ustadi

Hii ilikuwa nguo iliyo tengenezwa kwa nyuzi mtu aliyo sokotwa pamoja kufanya uzi mgumu.

kilemba

kitambaa kirefu cha kichwa kinacho zungushwa kichwani mara kadhaa.

taji takatifu

Hili taji limeelezewa katika 29:5 kuwa limechorwa kwa maneno "tolewa kwa ajili ya Yahweh"

Exodus 29:8

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa.

walete hao wanawe

"walete wana wa Aruni"

kanzu

Hili lilikuwa kanzu lilo shoneshewa mchoro.

mshipi

kipande cha kitambaa watu wanacho vaa kwenye kiuno au kwenye kifua.

kofia

Kofia hii ni nyembamba, ya urembo ambayo mtu ni kitambaa mtu anacho vaa kichwani juu ya macho.

kwa kazi takatifu

"wajibu wa kuwa makuhani"

watakuwa na huo

Wajibu wa kuwa makuhani pia utakuwa na zao la wana wa Aruni.

amri ya milele

"sheria isiyo na mwisho"

Exodus 29:10

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa.

hema ya kukutania

Hili ni jina lingine la maskani.

Kisha utamchinja huyo ng’ombe

Sadaka ya ng'ombe ilikuwa ichinjwe na Musa, na sio makuhani, njiani mwa mlango, sio ndani ya hema la kukutania.

Exodus 29:12

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kungea na Musa.

pembe

Hii ilikuwa mifano ya pembe za ng'ombe zilizokuwa zimewekwa kwenye miisho minne ya madhabahu.

damu yote

"damu iliyo baki"

yafunikayo matumbo

"yanayofunika viungo vya ndani"

ini ... figo

Hivi ni viungo mwilini.

Lakini nyama yake huyo ng’ombe, na ngozi yake, na mavi yake

"Lakini kwa viungo vilivyo baki vya ng'ombe"

Exodus 29:15

Pia mtwae kondoo

Kwa hizi dhabihu za kutengwa za makuhani, alikuwa Musa, sio Aruni wala wana wake, aliye hua wanyama.

katika madhabahu

Tofauti na sadaka ya ng'ombe iliyo chomwa nje ya hema, kondoo allichomwa katika madhabahu ya ndani.

matumbo yake

"viungo vya ndani"

Exodus 29:19

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa.

Kisha utamchinja kondoo

Kondoo aliuliwa kwa kukata koromeo lake.

Exodus 29:21

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa.

Exodus 29:22

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa.

matumbo ... ini ... figo

Hivi ni viungo vya ndani.

Utwae na mkate mmoja ... mbele ya Yahweh

Kwa ajili ya 29:23 ona jinsi ulivyo tafsiri maneno kama hayo 29:1

Exodus 29:24

Maelezo ya Jumla

Mungu anaendelea kuongea na Musa.

Nawe utavitia hivi

Hapa "hivi" lina husu sehemu za dhabihu vilivyo tajwa katika mistari ya awali.

ni sadaka iliyotengenezwa kwangu kwa njia ya moto

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 29:26

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa.

kondoo wa kuwekwa

"kondoo uliye mtoa" au "kondoo uliye muua"

kondoo wa kuwekwa kwake Haruni

"kondoo uliye kuwa ukimwekea Aruni"

Exodus 29:29

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa.

Na hayo mavazi matakatifu ya Aruni yatakuwa ya wanawe baada yake

Haya mavazi yalikuwa ni ya kikuhani ni sio ya Aruni peke yake.

wayavae watakapotiwa mafuta, na watakapowekwa kwa kazi takatifu

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

hema ya kukutania

Hili ni jina llingine la maskani.

Exodus 29:31

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa.

kondoo mume aliyekuwa wa kuwekwa kwa kazi takatifu

"kondoo uliye muua kwa kazi takatifu"

katika mahali patakatifu

Hii sio mahali patakatifu njee na mahali patakatifu

hema ya kukutania

Hili ni jina lingine la maskani.

havitaliwa

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

maana, ni vitu vitakatifu

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 29:35

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa.

Ni hivyo utakavyowatendea Aruni na wanawe kama nilivyo kuagiza

"Nimekuamuru kumtendea Aruni na wana wake hivi"

Exodus 29:38

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa.

Lazima utoe kwenye madhabahu wana-kondoo wa mwaka mmoja wawili siku baada ya siku

"Kila siku utoe sadaka katika madhabahu"

Exodus 29:40

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa.

vibaba vitatu ... kibaba na robo

"1/10 ... 1/4"

kibaba

kibaba ni lita 22.

Exodus 29:41

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa.

ni dhabihu ya kusongezwa kwangu kwa njia ya moto

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

katika vizazi vyenu vyote

"katika vizazi vyote vya uzao wenu"

hema ya kukutania

Hili ni jina lingine la maskani.

Exodus 29:43

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa.

na hiyo hema itafanywa takatifu na utukufu wangu

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 29:45

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa.

Exodus 30

Exodus 30:1

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa jinsi ya kujenga vifaa vya kuabuduia.

Nawe fanya

Hapa "nawe" ya husu Musa na watu wa Israeli.

pembe zake zitakuwa

Hizi zilikuwa mifano ya pembe za ng'ombe zilizo wekwa kwenye miisho ya madhabahu.

Exodus 30:3

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini watu wake wafanye.

utazifanya

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 30:5

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa nini watu wafanye.

sanduku la ushuhuda

Sanduku ni chombo chenye zile amri.

nitakapokutana nawe

Hapa "nawe" ya husu Musa.

Exodus 30:7

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa nini watu wafanye.

katika vizazi vyenu vyote

"katika vizazi vya uzao wenu wote"

Exodus 30:10

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa.

pembe

Hizi zilikuwa mifano iliyo onekana kama pembe za ng'ombe zilizo katika miisho minne ya madhabahu.

katika vizazi vyenu vyote

"katika vizazi vyote vya uzao wenu"

Exodus 30:11

Utakapowahesabu wana wa Israeli

Viongozi waliwahesabu wanaume tu.

Kila mtu apitaye kwa wale waliohesabiwa

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji. Walihesabu wanaume tu.

nusu shekeli

"1/2 shekeli"

gera ishirini

"20 gera"

miaka ishirini, au zaidi

Namba kubwa zinaongelewa kwa kuwa juu au juu ya namba ndogo.

Exodus 30:15

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa nini watu wafanye.

Watu

Wanaume tu walifanya hii sadaka.

Ili kwamba ziwe ukumbusho kwa ajili ya wana wa Israeli mbele yangu ili kufanya upatanisho kwa ajili ya roho zenu

Maana zinazo wezekana ni 1) "itawakumbusha Waisraeli kufanya upatanisho kwa ajili ya roho zao" au 2) "itawakumbusha Waisraeli wamefanya upatanisho kwa ajili ya roho zao"

Exodus 30:17

birika

"bakuli"

tako lake la shaba

Hili ndilo litakalo wekewa bakuli.

ili kuogea

Hili neno la elezea nini makuhani walitumia bakuli kubwa kwa ajili gani.

madhabahu

madhababu ya sadaka

Exodus 30:19

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa nini watu wafanye.

kwake yeye na kwa wazao wake katika vizazi vyao vyote

"kwa Aruni na vizazi vyote vya uzao wake"

Exodus 30:22

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa nini watu wafanye.

manukato

mimea iliyo kauka watu wanayo kausha kuwa unga na kuweka kwenye mafuta au chakula kutoa harufu nzuri au ladha.

shekeli mia tano ... shekeli 250

"shekeli 500 ... shekeli 250" Shekeli ni kama gramu 11.

mdalasini ... kane ... kida

Haya ni manukato mazuri.

kwa kuiandama shekeli ya mahali patakatifu

Dhahiri kulikuwa na shekeli zenye uzito zaidi ya moja kipindi hicho.

kazi ya ustadi ya mtengezaji manukato

Maana zinazo wezekana ni 1) Musa alikuwa na mtengeneza manakuto afanye hii kazi au 2) Musa alikuwa afanye hii kazi kama mtengeneza manukatao anavyo fanya.

mtengezaji manukato

mtu mwenye utaalamu wa kuchanganya manukato na mafuta

Exodus 30:26

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa.

Nawe utaipaka

Hapa "nawe" ya husu Musa.

sanduku la ushuhuda

Sanduku ni chombo chenye amri.

madhabahu ya kufukizia uvumba

"madhabahu ambayo sadaka ziliteketezwa"

Exodus 30:29

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa.

utavitakasa

Hii ya husu vitu vilivyo orodheshwa 30:26

katika vizazi vyenu vyote

"vizazi vyote vya uzao wenu"

Exodus 30:32

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa nini watu wafanye.

Hayatamiminwa katika kiwiliwili cha binadamu

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

mfano wa haya

"kwa viungo hivyo" au "kwa vitu hivyo"

mtu huyo atakatiliwa mbali na watu wake

Umbo "katiliwa" lina maana sio chini ya tatu. Inaweza elezewa katika tensi tendaji. 1) "hatahesabiwa kuwa moja wa watu wa Israeli" 2)"watu wa Israeli lazima wamuondoe" au 3) "watu wa Israeli lazima wa muue"

Exodus 30:34

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa nini cha kufanya. Yahweh anampa amri Musa tu.

natafi, na shekelethi, na kelbena

Haya ni manukato.

Nawe utafanya uvumba wa vitu hivyo, manukato ya kazi ya ustadi wa mtengenazaji manukato, yatakuwa yamekolea

Neno "yamekolea" la weza tafsiriwa katika tensi tendaji.

mtengenazaji manukato, yatakuwa yamekolea

Maana zinazo wezekana ni 1) Musa alipaswa kumpa mtengeneza manukato kufanya kazi au 2) Musa alipaswa kufanya kazi peke yake.

utayaponda

"utasaga"

Exodus 30:37

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa nini watu wafanye.

hamtajifanyia

Hii ya husu watu wa Israeli.

sawasawa

"kwa viungo kama hivyo"

utakuwa kwenu mtakatifu

"Utahesabu kuwa takatifu"

atakatiliwa mbali na watu wake

Umbo "katiliwa" lina maana sio chini ya tatu. Inaweza elezewa katika tensi tendaji. 1) "hatahesabiwa kuwa moja wa watu wa Israeli" 2)"watu wa Israeli lazima wamuondoe" au 3) "watu wa Israeli lazima wa muue"

Exodus 31

Exodus 31:1

nimemwita kwa jina

Mungu anzungumza kuchagua watu maalumu kwa kuwaita majina yao.

Bezaleli ... Uri ... Huri

Haya ni majina ya wanaume.

Exodus 31:3

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuzungumza na Musa.

nimemjaza Bezaleli na roho ya Mungu

Yahweh anazungumza kumpa Bezaleli Roho yake kana kwamba Bezaleli ni birika na Roho ya Mungu ni maji.

Exodus 31:6

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuzungmza na Musa.

Oholiabu ... Ahisamaki

Haya ni majina ya wanaume.

Nami nimetia hekima katika mioyo ya wote wenye moyo wa hekima

Mungu anazungumza kufanya watu kuweza kutengeneza vitu kana kwamba uwezo alikuwa anaweka kwenye mioyo yao.

hema la kukutania

Hili ni jina lingine la maskani.

sanduku la ushuhuda

Sanduku ni chombo kinacho hifadhi amri.

madhabahu ya kufukizia uvumba

"madhabahu ya kuteketeza uvumba"

madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa

"madhabahu ambayo sadaka ili teketezwa"

Exodus 31:10

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuzungumza na Musa.

mavazi yenye kufumwa kwa uzuri

Hii ilikuwa nguo iliyo tengenezwa kwa nyuzi mtu aliyo sokotwa pamoja kufanya uzi mgumu.

Exodus 31:12

Hakika mtazishika Sabato zangu

Mungu anazungumza kutii maelekezo yake kuhusu Sabato kama kushika Sabato.

kati ya mimi na ninyi katika vizazi vyenu vyote

"kwa vizazi vyote vya uzao wenu"

niwatakasaye ninyi

Mungu anaongelea kuchagua kuwa wake kwa kuwatenga kwake.

ni takatifu kwenu

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

kila mtu atakayeitia unajisi

Mungu anazungmzia kutoheshimu Sababto kama kuinajisi.

hakika yake atauawa

"lazima hakika auawe" Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

itakatiliwa mbali na watu wake

Umbo "katiliwa" lina maana sio chini ya tatu. Inaweza elezewa katika tensi tendaji. 1) "hatahesabiwa kuwa moja wa watu wa Israeli" 2)"watu wa Israeli lazima wamuondoe" au 3) "watu wa Israeli lazima wa muue"

lakini siku ya saba

"lakini siku ya 7"

Exodus 31:16

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa nini awaambie watu wa Israeli.

wataishika Sabato

Mungu anaongelea kutii maelekezo yake kuhusu Sabato kama kushika Sabato.

Kuiangalia sana hiyo Sabato katika vizazi vyao vyote

"Wao na vizazi vyote vya watu wao wa itunze"

agano la milele

"sheria isiona mwisho"

Exodus 31:18

zilizoandikwa kwa mkono wake

Hii yaweza tafsiriwa kwa tensi tendaji.

Exodus 32

Exodus 32:1

watu walipoona

Hapa kuelewa kitu kuna zungumziwa kama kinaonekana.

Njoo, katufanyizie sanamu

Neno "njoo" lina imarisha nguvu ya agizo linalo fuata. Watu walikuwa wanataka Aruni awafanyie sanamu kwa ajili yao.

itakayokwenda mbele yetu

"tuongoza sisi" au "kuwa kiongozi wetu"

mkaniletee

Neno "wao" la husu pete za dhahabu.

Exodus 32:3

Watu wote

Hii ya husu watu wote waliyo mkataa Musa kama kiongozi wao na Mungu wa Musa kama Mungu wao.

akaitengeneza kwa patasi, akaifanya iwe sanamu ya ndama kwa kuiyeyusha

Aruni aliyayusha dhahabu na kumimina kwenye patasi iliyo kuwa na umbo la ndama. Dhahabu ilipo kuwa ngumu, aliondoa patasi, na dhahabu iliyo ngumu ikawa na umbo la ndama.

Exodus 32:5

Haruni alipoona jambo hili

"Aruni alipoona kile watu walicho fanya"

wakaondoka wacheze

"kuwa na sherehe ya kukithiri." Watu yawezakana walifanya matendo ya kimapenzi ya kuchukiza.

Exodus 32:7

Wamepotoka upesi kuiacha ile njia niliyowaamuru

Hapa Mungu anaongelea watu kutotii alicho waamuru kana kwamba aliwaambia waenende kwenye njia maalumu na wakaiacha.

wamejifanyizia ndama ya kuyeyusha

"Wamefanya sanamu ya dhahabu iliyo kama ndama"

Exodus 32:9

Mimi nimewaona watu hawa

Hapa Yahweh analinganisha kuwajua watu na kuwaona.

watu wenye shingo ngumu

Yahweh anaongelea watu kuwa wajehuri kana kwamba wana shingo ngumu.

Basi sasa

Neno "sasa" linatumika hapa kuweka pumziko kwa kile Yahweh alikuwa anamwambia Musa. Hapa Yahweh anasema nini ata wafanyia watu.

hasira zangu ziwake juu yao

Yahweh anazungumzia hasira yake kana kwamba ni moto unao weza waka sana.

wewe uwe

Neno "wewe" la husu Musa.

kwa nini hasira zako kuwaka juu ya watu wako

Musa alitumia ili swali kujaribu kumshawishi Yahweh asiwe na hasira sana na watu wake.

uweza mkuu ... mkono wenye nguvu

Hii mistari miwili ina maana moja na iwe ambatanishwa kwa mkazo.

Exodus 32:12

Maelezo ya Jumla

Musa anaendelea kujadiliana na Mungu asiharibu Israeli.

Kwa nini Wamisri kusema, 'Amewatoa ... kuwaondoa watoke juu ya uso wa nchi?'

Musa ametumia ili swali kumshawishi Mungu asiharibu watu wake.

uso wa nchi

"kutoka kwneye uso wa dunia" au "kutoka kwenye dunia"

Geuka katika hasira yako kali

"acha hasira yako kali" au "acha kuwa na hasira sana"

hasira yako kali

Musa anazungumzia hasira ya Mungu kana kwamba ni moto uliyo kuwa wa waka.

Mkumbuke Ibrahimu

"Fikiria kuhusu Ibrahimu"

kuwaambia

"alifanya nadhiri"

watairithi milele

Mungu anazungumzia kuhusu wao miliki nchi kana kwamba watairithi.

Exodus 32:15

mbao mbili za mawe

Hizi ni mbao mbili za mawe ambazo Mungu aliandika amri zake.

Na zile mbao zilikuwa kazi ya Mungu nayo maandiko yalikuwa maandiko ya Mungu

Hii mistari miwili ina maana moja. Wa pili waeleza jinsi hizi mbao zilikuwa "kazi pekee ya Mungu"

Exodus 32:17

akamwambia Musa

Ina kadiriwa kuwa Yoshua alikutana na Musa wakati Musa akirudi kambini.

Exodus 32:19

zile mbao

"zile mbao mbili Yahweh alizo ziandikia"

Exodus 32:21

Musa akamwambia Aruni, "Watu hawa ... dhambi hii kuu juu yao?

Hii yaweza andikwa kama nukuu isiyo ya moja kwa moja.

ukaleta dhambi hii kuu juu yao?

Musa aliongea kusababisha watu kufanya dhambi kana kwamba dhambi ni kitu na Aruni aliwawekea.

Hasira yako isiwake

Aruni aliongelea hasira ya Musa kana kwamba ni moto unao weza kuchoma. "Usiwe na hasira sana"

wamejielekeza kwa mabaya

Kupania kufanya uovu kunaongelewa kama kuwekwa kwenye uovu.

huyo Musa

Watu walionyesha kutoheshimu kwa kuweka "huyo" kabla ya jina lake, kana kwamba Musa laikuwa mtu wasio mjua na hawawezi muamini.

Nikawaambia, 'Mtu ye yote aliye na dhahabu na aivue

Hii yaweza andikwa kama nukuu isiyo ya moja kwa moja.

nikaitupa ndani ya moto, akatoka ndama huyu

Badala ya kuchukuwa umiliki wa kutengeneza ndama, Aruni anadai ndama alitoka kwenye moto kimuujiza.

Exodus 32:25

wameasi

"walikuwa wanatenda kinyama" au "hawakuwa wanajizuia"

Ndipo Musa akasimama katika mlango ... "Mtu awaye yote aliye upande wa Yahweh na aje kwangu."

Hii yaweza andikwa kama nukuu isiyo ya moja kwa moja.

Mtu awaye yote aliye upande wa Yahweh

Musa anazungumza kwa mwaminifu kwa Yahweh kama kuwa upande wa Yahweh.

akapite huko na huko toka mlango hata mlango

"nenda ndani na nje kutoka mlango mmoja wa kambi kwenda mwingine"

Exodus 32:28

watu elfu tatu

"watu 3000"

kila mtu juu ya mwanawe na juu ya ndugu yake

Ukweli kwamba wamefanya hivi kwa kutomtii Mungu yaweza andikwa kwa wazi.

Exodus 32:30

Mmetenda dhambi kuu

Waliabudu sanamu.

Labda nitafanya upatanisho kwa ajili ya dhambi yenu

Musa aliongea kumshawishi Mungu kuwasamehe watu kana kwamba aliweza fanya upatanisho kwa ajili ya dhambi.

unifute, nakusihi, katika kitabu

Hapa Musa anaongelea jina lake.

kitabu chako ulichoandika

Mungu alicho andika katika kitabu cha weza andikwa wazi.

Exodus 32:33

Mtu ye yote aliyenitenda dhambi ndiye nitakayemfuta katika kitabu changu

Maneno "mtu ye yote" ya wakilisha "hilo jina la mtu"

kitabu changu

Hii ya husu kitabu cha Yahweh Musa alicho zungumzia katika 32:30

Yahweh akawapiga hao watu

Hili pigo la weza kuwa ugonjwa mkali.

alivyoifanya ile ndama, ambayo Aruni aliifanya

Japo kuwa Aruni alifanya ndama, watu walikuwa na hatia kwasababu walimwambia Aruni afanye.

Exodus 33

Exodus 33:1

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa hasira yake.

hiyo nchi, inayo tiririka kwa maziwa na asali

Nchi ilikuwa nzuri kwa kufuga mifugo na kuotesha mazao.

inayo tiririka

"imejawa na" au "yenye utele wa"

maziwa

Sababu maziwa yanatoka kwa ng'ombe na mbuzi, hii inawakilisha chakula cha mifugo.

asali

Sababu asali inatokana na mahua, hii inawakilisha chakula cha mazao.

watu wajehuri

"watu wanao goma kubadilika"

Exodus 33:4

mikufu

nguo nzuri pamoja na mikufu na pete yenye madini ndani yake

watu wajehuri

"watu wanao goma kubadilika"

Exodus 33:7

nguzo ya wingu

Wingu lilikuwa na umbo la nguzo.

ilishuka chini

Lilipo shuka kutoka yaweza andikwa wazi.

Exodus 33:10

Yahweh alizungumza na Musa uso kwa uso

Kuzungumza moja kwa moja pasipo ndoto na maono, inaongelewa kana kwamba Musa na Mungu walionana uso walipo ongea.

kijana

mkubwa wakutosha kuwa mwanajeshi (17:8), lakini mdogo kwa Musa

Exodus 33:12

Ona

"Tazama!" au "Sikia!" au "Kuwa makini kwa nitakalo kwambia."

Nina kujua kwa jina

Kumjua mtu kwa jina ni kumjua vizuri.

umepata upendeleo kwangu

Hii ni moja ya ambacho Mungu alimwambia Musa.

Kama nimepata upendeleo machoni pako

Hii ni moja ya Musa aliyo mwambia Mungu.

nionyeshe njia zako

Maana inayo wezekana ni 1) "nionyeshe unacho kwenda kufanya mbeleni" au 2) "nionyeshe jinsi watu wanawezaje kufanya yanayo kupendeza"

Exodus 33:14

Uwepo wangu utaenda

"Uwepo wa Mungu una muwakilisha yeye"

utaenda nawe ... nitakupa

Neno "nawe" lina husu Musa.

nitakupa pumziko

"Nitaacha upumzike"

Au je

"Kama uwepo husipo enda nasi"

itajulikanaje

Hii yaweza elezwa kwa tensi tendaji.

itajulikanaje

Musa alitumia hili swali kusisitiza kwamba kama Mungu hasipo enda nao, hakuna mtu atakaye jua kuwa Musa kapata upendeleo machoni pa Mungu.

Haitakuwa kuwa tu kama

"Haitajulikana tu kuwa kama"

Exodus 33:17

Maelezo ya Jumla

Yahweh anapo tumia neno "nawe" katika huu mstari, ni katika uchache na lina husu Musa.

umepata upendeleo machoni mwangu

Huu ni msemo wenye maana kwamba Mungu kapendezwa naye.

nina kujua kwa jina

Kumjua mtu kwa jina ni kumjua vyema.

Exodus 33:19

Nitafanya wema wangu wote ujulikani kwako

Mungu anaongelea kutembea mbele ya Musa ili Musa aone wema kana ni wema wake tu utakao pita kwa Musa.

Exodus 33:21

Ona

"Tazama!" au "Sikia!" au "Kuwa makini kwa nitakacho kwambia"

utaona mgongo wangu

Hii ni kwasababu Yahweh atakuwa akiondoka kwa Musa.

ila uso wangu hautaonekana

Hii yaweza elezezwa katika tensi tendaji.

Exodus 34

Exodus 34:1

mbao

"mbao za mawe"

Exodus 34:3

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa

Usiruhusu mtu yeyote aonekana popote kwenye mlima

Kuonekana kufanya kitu ya wakilisha kufanya hicho kitu.

Hakuna kundi la mifugo wanao ruhusiwa ata kula mbele ya mlima

"Ata mifugo hawaruhusiwi kuja karibu na mlima kula"

Exodus 34:5

akasima mbele za Musa

"akasimama na Musa katika mlima"

akatamka jina "Yahweh"

Maana zinazo wezekana ni 1) "alitaja jina "Yahweh"' au 2) "alikiri Yahweh ni nani." Kwa maana ya pili, "jina" lina wakilisha Mungu ni nani.

Yahweh, Yahweh, Mungu ni wa rehema na wa neema

Mungu anaongea kuhusu yeye.

anadumu katika uwaminifu wa agano na uadilifu

"mara zote anaonyesha uwaminifu wa agano na uadilifu"

anadumu katika uwaminifu wa agano

"mara zote ni mwaminifu wa agano langu"

anadumu katika ... uadilifu

"mara zote uwa mwadilifu"

Lakini

Yahweh anazungmza kuhusu yeye.

hamsafishi mwenye hatia

Yahweh anazungmza kuhusu yeye.

hamsafishi mwenye hatia

"hakika hasafishi mwenye hatia" au "hakika hatasema kwamba mwenye hatia hana makosa" au "hata wa weka huru watu wenye hatia"

Ataleta adhabu ya dhambi za baba kwa watoto wao

Kutoa hadhabu kuna ongelewa kana kwamba hadhabu ni kitu mtu anaweza kuleta kwa watu.

watoto wao

Neno "watoto" la wakilisha uzao.

Exodus 34:8

Kama sasa nimepata upendeleo machoni pako

Kumpendeza mtu kuna zungumziwa kama kupata upendeleo machoni pao.

maasi yetu na dhambi zetu

Maneno "maasi" na "dhambi" kimzingi ina maana moja na yame unganishwa kwa msisitizo.

utuchukuwe kama urithi wako

Kitu ambacho mtu ana miliki milele kina zungumziwa kana kwamba ni kitu mtu alirithi.

Exodus 34:10

watu wako

Hapa "wako" ya husu Musa.

ni kitu cha hofu ninacho fanya kwako

Kitu cha hofu ni kitu kinacho sababisha watu kuogopa. Katika hoja hii, watu watamuogopa Mungu watakapo ona anacho fanya.

ninacho fanya kwako

Hapa "kwako" ya husu Musa na watu wa Israeli.

Exodus 34:12

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa. Hapa ana mwambia nini Musa na watu wafanye.

wata kuwa mtego kwako

Watu wanao jaribu wengine kufanya dhambi wana zungumziwa kama ni mtego.

ambaye jina lake ni Uwivu

Neno "jina" hapa la wakilisha tabia ya Mungu.

Yahweh, ambaye jina lake ni Uwivu

Neno "Uwivu" hapa lina maana ya kuwa Mungu anajali kutunza hesima yake. Kama watu wake wakiabudu miungu mingine, ana poteza heshima, kwasababu watu wasipo muheshimu, watu wengine pia hawata muheshimu.

Exodus 34:15

Sentensi Unganishi

Yahweh anaendelea kumwambia Musa jinsi watu wake wana paswa kutenda kwa watu wa njee.

kwa kuwa wanajifanyia ukahaba kwa miungu yao

Mungu anaongelea watu wengine kuabudu miungu mingine kana kwamba ni makahaba wanaenda kwa wanaume wengine.

na wewe utakula baadhi ya dhabihu zake

Madhara ya kula chakula kilicho tolewa dhabihu kwa mungu mwingine yaweza andikwa wazi.

Exodus 34:18

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa nini watu wafanye.

siku saba

"siku 7"

mwezi wa Abibu

Hili ni jina la mwezi wa kwanza wa kalenda ya Kiebrania. Abibu ni wakati wa sehemu ya mwisho ya Machi na sehemu ya kwanza ya Aprili kwa kalenda za Magharibi.

Exodus 34:19

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa nini watu wafanye.

umnunue tena

Wazaliwa wa kwanza na wazaliwa wa kwanza wa punda walikuwa ni wa Yahweh, lakini Yahweh Yahweh hakutaka watolewe dhabihu kwake. Badala yake, Waisraeli walikuwa watoe dhabihu ya kondoo katika nafasi yake. Hii ili waruhusu Waisraeli kununua punda na wanao kutoka kwa Yahweh.

Hakuna ata mmoja atakye kuja kwangu mikono mitupu

Mungu anaongelea sadaka kana kwamba mtu alikuwa abebe mikononi mwake.

Exodus 34:21

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa nini watu wafanye.

Ata wakati wakilimo na wa mavuno

"Ata unapo andaa ardhi au kukusanya mazao"

Sherehe ya Makusanyo

Sherehe ilijulikana kama pia Sherehe ya Mahifadhi au Sherehe ya Mabanda. Wazao lilikuja kutoka kwa walimaji walipo ishi kwenye vibanda vya muda mfupi, au nyumba za nyasi, nje kwenye mashamba kulinda mazao yanapo komaa. Neno "Makusanyo" ina maana wanapo vuna mazao yao.

Exodus 34:23

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa nini watu wafanye.

Exodus 34:25

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa nini watu wafanye.

damu ya dhabihu yangu

Ukweli kwamba damu ni ya wanyama ina weza andikwa wazi.

hamira yeyote

Ukweli kwamba hamira ye yote yaweza kuwa kwenye mkate yaweza andikwa wazi.

Exodus 34:27

Musa alikuwa huko

"Musa alikuwa kwenye mlima"

siku arobaini

"siku 40"

siku arobaini na usiku

"kwa siku arobaini, mchana na usiku"

Aliandika

"Musa aliandika"

Exodus 34:29

ulikuwa wa'ngaa

"ulianza kuwaka"

wakaja kwake

"wakamfuata" au "wakamuendea." Hawa kwenda kwenye mlima juu.

Exodus 34:32

amri zote Yahweh alizo mpa

Kutoa amri kuna zungumziwa kana kwamba amri zilikuwa ni vitu vinavyo weza kutolewa.

Exodus 34:34

aliondoa

"Musa aliondoa"

alicho amriwa

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 35

Exodus 35:1

siku ya saba

"siku ile ya saba" au "Juma mosi"

Yeyote atakaye fanya kazi hiyo siku lazima auawe

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 35:4

Maelezo ya Jumla

Musa akawambia Waisraeli wafanye vitu Yahweh alivyo muamuru katika 25:3

Chukuwa sadaka kwa ajili ya Yahweh

"Chukuwa matoleo kwa ajili ya Yahweh"

wote wenye moyo mkunjufu

Hapa "moyo" ya husu mtu anaye leta sadaka.

Exodus 35:10

Maelezo ya Jumla

Musa anaendelea kuwaambia watu nini Mungu kawaamuru kufanya.

Kila mwanaume mwenye ustadi

"Kila mwanaume aliye na ustadi"

vifungo

Vifungo vinatoshea kwenye vishimo vyake kushikilia pazia pamoja.

sakafu

Hivi ni vitu vizito vinavyo kaa chini na kuwezesha visisogee.

kiti cha rehema

Hichi ni kiti kinacho keti juu ya sanduku ambapo sadaka ya upatanisho yatolewa.

Exodus 35:13

Walileta

"Watu wa Israeli walileta"

mkate wa wonyesho

Huu mkate uliwakilisha uwepo wa Mungu.

kitunzi cha shaba

Hii ni fremu ya chuma za shaba za kushikilia mbao zinapo chomeka.

Exodus 35:17

vishikizo

Hizi zilikuwa pazia kubwa zilizo tengenezwa kwa kitambaa.

nguzo

Hizi zilikuwa vipande vigumu vya mbao vilivyo nyooshwa na kutumika kama vishikizo.

sakafu

Hizi zilikuwa tofali zenye shikizo ndani yake kushikilia mbao.

misumari ya hema

vipande vikali vya mbao au chuma vilivyo tumika kuhifadhi miisho ya hema kwenye ardhi.

Exodus 35:20

makabila yote ya Israeli

Hii ya husu watu katika makabila.

mtu moyo wake ulimchochea

Hapa "moyo" wa husu mtu. Moyo uliyo mjibu Mungu unazungumziwa kana kwamba ni maji yaliyo tibuliwa na mafuriko.

aliye andaliwa na roho yake

Hapa "roho" ya husu mtu.

wote waliokuwa na moyo wa utayari

Hapa "moyo" wa husu mtu.

madini, hereni, pete, na vitu vya thamani

Hizi ni aina ya mikufu.

Exodus 35:23

Kila mmoja alikuwa na ... walivileta

Kwa 35:23 ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno katika 25:3

Exodus 35:25

buluu, dhambarau, au sufu nyekundu

Maana zinazo wezekana ni 1) "vitu vilivyo tiwa buluu, zambarau, na sufu nyekund," 2) "buluu, zambarau na iliyo tiwa sufu nyekundu"

wenye mioyo iliyochochewa

Hapa "mioyo" ya husu wanawake. Mioyo ya wanawake iliyo mjibu Mungu inazungumziwa kana kwamba ni maji yaliyo tibuliwa na mafuriko.

Exodus 35:27

Viongozi walileta

Kwa 35:27-29 ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno katika 25:1 na 25:3

ambao mioyo yao ilikuwa tayari

Hapa "moyo" wa husu Musa.

Exodus 35:30

Aliijaza Bezaleli kwa Roho yake

Roho wa Mungu aliye mpa Bezaleli uwezo wa kufanya kazi una ongelewa kama kama kitu kilicho mjaza Bezaleli.

ubunifu na ujenzi

Kwa 35:30-33 ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno.

Exodus 35:34

Maelezo ya Jumla

Musa anaendelea kuongea na watu.

Aliiweka kufundisha ndani ya moyo wake

Hapa "moyo" wa husu Bezaleli. Uwezo wa kufundisha unazungumziwa kana kwamba ni kitu kinachoweza kuwekwa kwenye moyo.

Aliwajaza kwa ustadi

Ustadi wa kutengeneza vitu vizuri unazungumziwa kana kwamba ni kitu kinacho weza kumjaza mtu.

Oholiabu mwana wa Ahisamaki, kutoka kabila la Dani

"Oholiabu" na "Ahimasaki" ni majina ya wanaume.

mwerevu

mtu anaye kata michora kwenye vitu vigumu kama mbao, mawe, au chuma

washonaji

mtu anaye tengeneza nguo kutumia uzi

wabunifu wa sanaa

mtu anaye tengeneza uzuri kwa vifaa

Exodus 36

Exodus 36:1

Maelezo ya Jumla

Musa anaendelea kuongea na watu.

Bezaleli

Hili ni jina la mwanaume.

Oholiabu

Hili ni jinala mwanaume

ambaye Yahweh aliye mpa ustadi na uwezo

Hapa ustadi na uwezo unaongelewa kana kwamba ni kitu Yahweh anacho weza kuweka ndani ya mtu

kadiri ya yote Yahweh aliyo amuru

"kama Yahweh alivyo amuru"

Exodus 36:2

Bezaleli

Hili ni jinala mwanaume

Oholiabu

Hili ni jinala mwanaume

ambaye moyoni mwake ulichochewa

Hapa "moyo" una husu mtu. Moyo uliyo mjibu Mungu unaongelewa kana kwamba ni maji yaliyo tibuliwa na mafuriko.

Exodus 36:5

Wachonga mawe walimwabia Musa ... aliyo tuamuru

Hii yaweza andikwa kama nukuu ya moja kwa moja.

Wachonga mawe walimwabia Musa

"Wanaume walikuwa wanafanya kazi ndani ya hekalu walimwambia Musa"

Exodus 36:8

Hivyo wachonga mawe ... akaviunganisha pamoja

Kwa 38:8-10 ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno kwenye 26:1

mapazia kumi yaliyo jengwa kitamba kizuri

Haya mapazia ni vipande vya nguo vilivyo shonwa na pomaja ili viweze kuunda ukuta au hema

Bezaleli

Hili ni jinala mwanaume

Exodus 36:11

Kisha akafanya vitanzi ... ikawa maskani moja

Kwa 36:11-13 ona jinsi ulivyo tafsiri maneno haya 26:4

vitanzi vya uzi wa bluu

vitanzi vya vitambaa vya bluu

kitambaa

Haya yalikuwa vitambaa vikubwa vya kushona vilivyo tumika kutengeneza kifuniko na kuta za kugawanya patakatifu.

Akafanya

Hapa "akafnya" ya husu Bezaleli, lakini ina husisha wanaume wanao fanya kazi hekaluni.

kulabu hamsini za dhahabu

"kulabu 50 za dhahabu"

Exodus 36:14

Bezaleli akafanya vitambaa ...

Kwa 36:14-17 ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno katika 26:7 na 26:10

kumi na moja ndivyo alivyofanyiza

"alifanya 11"

mikono thelathini

"mikono 30"

vitanzi hamsini

"vitanzi 50"

Exodus 36:18

Bezaleli akafanya ... upande wa juu

Kwa 36:18-19 ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno katika 26:10 na 26:12

kulabu hamsini za shaba

"kulabu 50 za shaba"

Exodus 36:20

Bezaleli akafanya ... kwa ajili ya upande kuelekea kusini

Kwa 36:20-23ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno katika 26:15

mikono kumi ... mkono mmoja na nusu

"mikono 10" ... 1.5"

ndimi mbili zilizounganishwa

Ndimi ni kipande kidogo cha mbao kinacho tokeza mwisho wa mbao ilikuwa salama

Exodus 36:24

Bezaleli akafanya ...

Kwa 36:24-26ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno katika 26:19

vikalio arobaini vya fedha

"vikalio 40 vya fedha"

viunzi ishirini

"viunzi 20"

Exodus 36:27

Na kwa ajili ya zile pande za nyuma ... ya maskani

Kwa 36:27-28 ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno katika 26:22

kuelekea magharibi

upande uliyo magharibi

kwenye pande zake mbili za nyuma

kwenye pande za nyuma ya maskani

Exodus 36:29

Hizi zilikuwa ...

Kwa 36:29-30 ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno katika 26:22

vikalio vyake kumi na sita

"vikalio vyake 16"

Exodus 36:31

Bezaleli akafanya

Kwa 36:31-34 ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno katika 26:26 na 26:29

magharibi

katika upande wa magharibi

mwisho mmoja mpaka ule mwingine

upande mmoja wa maskani kwenda mwingine

Exodus 36:35

Bezaleli akafanya ... vikalio vinne vya fedha

Kwa 36:35-36 ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno katika 26:31

Exodus 36:37

Naye akafanya ... vilikuwa vya shaba

Kwa 36:37-38 ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno katika 26:36

Naye akafanya

Hapa "naye" ya husu Bezaleli na wanao mfanyia kazi. "Bezaleli na wanaume wake wakafanya"

kisitiri

pazia

Exodus 37

Exodus 37:1

Bezalel

Hili lilikuwa jina la mwanaume.

Mikono miwili na nusu urefu

"mikono 2.5 ... mikono 1.5"

miguu yake minne

Hivi vipande viwili vya mbao vilivyo saidia sanduku vinazungumziwa kama ni mwanadamu au miguu ya mnyama.

Exodus 37:4

Maelezo ya Jumla

Kazi ya Bezaleli na kundi lake la endelea kujenga maskani na vivyombo vyake.

Kisha akafanya ... Mikono miwili na nusu

Kwa 37:4-6ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno katika 25:12 na 25:15

Kisha akafanya

Japo "akafanya" ya husu Bezaleli, "akafanya" yaweza husisha wafanya kazi wote waliyo msaidia.

Mikono miwili na nusu ... mkono mmoja na nusu

"mikono 2.5" ... mikono 1.5"

Exodus 37:7

Maelezo ya Jumla

Kazi ya Bezaleli na kundi lake la endelea kujenga maskani na vivyombo vyake.

Bezaleli akafanya ...

Kwa 37:7-9 ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno katika 25:15 na 25:19

Nao wakawa makerubi wanaonyoosha mabawa yao mawili kuelekea juu, wakisitiri

Bezaleli aliweka sanamu za makerubi kana kwamba walikuwa ni wa kweli waliyo nyoosha mabawa yao na na kusitiri kiti cha rehema.

Nyuso za makerubi hao zilielekea

Bezaleli aliweka sanamu za makerubi kana kwamba walikuwa ni wa kweli waliyo nyoosha mabawa yao na na kusitiri kiti cha rehema.

Exodus 37:10

Maelezo ya Jumla

Bazaleli na kundi lake wanaendelea kujenga maskani na vifaa.

Bezaleli akafanya ... ile miguu minne

Kwa 37:10-13 ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno katika 25:23 na 25:25

Mikono miwili ... mkono mmoja ... mkono mmoja na nusu

"mikono 2" ... mkono 1 ... 1.5"

upana wa kiganja

Huu ulikuwa upana wa mkono wa mwanaume na vidole vimetanuliwa

ile miguu minne

Hivi vipande vinne vya mbao vilivyo saidia sanduku vinazungumziwa kana kwamba ni mwanadamu au miguu ya mnyama.

Exodus 37:14

Maelezo ya Jumla

Bazaleli na kundi lake wanaendelea kujenga maskani na vifaa.

Pete hizo ... kutokana na dhahabu safi

Kwa 37:14-16 ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno katika 25:25 na 25:28

Pete hizo zilikuwa karibu

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

vyombo vilivyo juu ya meza, sahani zake na vikombe vyake na mabakuli yake na mitungi yake iliyotumiwa kumimina matoleo

Ni mabakuli pekee na mitungi inayo tumika kumimina matoleo.

Exodus 37:17

Sentensi Unganishi

Bazaleli na kundi lake wanaendelea kujenga maskani na vifaa.

Kisha akafanya ... yakitoka katika kile kinara cha taa

Kwa 37:17-19 ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno katika 25:31 na 25:33

na vikombe vitatu vyenye umbo la maua ya mlozi

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

maua ya mlozi

Maua ya mlozi ni meupe yenye mashina matano yanayo ota kwenye huo mti.

Exodus 37:20

Na kwenye kile kinara cha taa ... cha dhahabu safi.

Kwa 37:20-22 ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno katika 25:33 na 25:35

kulikuwa na vikombe vinne vyenye umbo la maua ya mlozi

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 37:23

Maelezo ya Jumla

Bazaleli na kundi lake wanaendelea kujenga maskani na vifaa.

Kisha akafanya ... talanta ya dhahabu safi

Kwa 37:23-24 ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno katika 25:37

vyetezo

Hichi ni kifaa kilicho tengenezwa kwa mifombo mbili au chuma iliyo unganishwa mwisho na kutumika kunyanyulia vitu.

talanta

"kilogramu 34"

Exodus 37:25

Maelezo ya Jumla

Bazaleli na kundi lake wanaendelea kujenga maskani na vifaa.

Sasa akafanya ... wa dhahabu

Kwa 37:25-26 ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno katika 30:1 na 30:3

Mkono

Mkono ni sentimita 46.

Pembe zake zilitoka kwake

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 37:27

Maelezo ya Jumla

Bazaleli na kundi lake wanaendelea kujenga maskani na vifaa.

Naye akaifanyia pete mbili za dhahabu ...

Kwa 37:27-28 ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno katika 30:3 na 30:5

kazi ya mtengenezaji wa marhamu

Mmarhamu ana ujuzi katika kuchanganya viungo na mafuta.

Exodus 38

Exodus 38:1

Maelezo ya Jumla

Bazaleli na kundi lake wanaendelea kujenga maskani na vifaa.

Naye akafanya ... Vyombo vyake vyote alivifanya kwa shaba

Kwa 38:1-3 ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno katika 27:1 na 27:3

Mikono

Mkona mmoja ni sentimita 46

Pembe zake zilitoka kwake

Hii yaweza andikwa tensi tendaji.

Exodus 38:4

Maelezo ya Jumla

Bazaleli na kundi lake wanaendelea kujenga maskani na vifaa.

Tena akaifanyia ... ile miti

Kwa 38:4-5 ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno katika 27:3 na 27:5

mtandao wa shaba

Hii yaweza tensi tendaji.

Exodus 38:6

Maelezo ya Jumla

Bazaleli na kundi lake wanaendelea kujenga maskani na vifaa.

Exodus 38:8

Maelezo ya Jumla

Bazaleli na kundi lake wanaendelea kujenga maskani na vifaa.

beseni ya shaba na kinara chake cha shaba

Kinara kilisaidia beseni ya shaba.

Kwa kutumia vioo

Shaba ilitoka kwa vioo.

vioo

Kioo ni kipande cha chuma kilicho ng'arishwa au glasi inayo onyesha umbo.

Exodus 38:9

Maelezo ya Jumla

Bazaleli na kundi lake wanaendelea kujenga maskani na vifaa.

Naye akafanya ... na viungo vyake vilikuwa vya fedha

Kwa 38:9-10 ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno katika 27:9

mia moja ... ishirini

"100 ... 20"

Mikono

Mkono ni sentimita 46.

Exodus 38:11

Pia, kwa ajili ya upande wa kaskazini ... viungo vyake vilikuwa vya fedha

Kwa 38:11-12 ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno katika 27:11

mikono mia ... ishirini ... hamsini ... kumi

"100 ... 20 ... 50 ... 10"

Mikono

Mkono ni sentimita 46

Exodus 38:13

hamsini ... kumi na mitano ... tatu

"50 ... 15 ... 3"

Mikono

Mkono ni sentimita 46

Mapazia yote ya ua kuzunguka pande zote yalikuwa ya kitani

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 38:17

Kwa 38:17-20 ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno katika 27:14 na 27:17

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Vibanio vya vikalio na viungo vyake vilikuwa vya fedha

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

kulikuwa na viungo vya shaba kwa ajili ya nguzo zote za ua

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

ishirini ... tano ... nne

"20 ... 5 ... 4"

Mikono

Mkono ni sentimita 46

utando wa vichwa vyake na viungo vyake ulikuwa wa fedha

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Na misumari yote ya hema kwa ajili ya maskani na kwa ajili ya ua kuzunguka pande zote ilikuwa ya shaba

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 38:21

Sentensi Unganishi

Bazaleli na kundi lake wanaendelea kujenga maskani na vifaa.

vilivyohesabiwa

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Ithamari

Hili ni jina la mwanaume.

Bezaleli mwana wa Uri mwana wa Huru

"Bezaleli" na "Uri" ni majina ya wanaume.

Yahweh alikuwa amemwamuru Musa

"kila kitu Yahweh alicho kuwa amemuamuru Musa kufanya"

Oholiabu mwana wa Ahisamaki

"Oholiabu" na "Ahisamaki" ni majina ya wanaume.

Exodus 38:24

Dhahabu yote iliyotumiwa kwa ajili ya kazi

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

alanta ishirini na tisa ... talanta mia moja

"talanta 29 ... talanta 100." Talanta ni kilogramu 34.

shekeli 730 ... shekeli 1,775

Shekeli ni gramu 11.

kulingana na shekeli ya mahali patakatifu

Ni wazi kulikuwa na shekeli zenye uzito zaidi ya moja kipindi hicho. Hii ili eleza ipi kutumika.

Nayo fedha ya wale walioandikishwa kati ya kusanyiko

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

nusu shekeli

"1/2 shekeli"

miaka ishirini

"miaka 20"

Exodus 38:27

Na talanta mia moja za fedha zilitumiwa kutengeneza

Talanta ni kilogramu 34.

mia moja ... sabini

"100 ... 70"

shekeli

Shekeli ni gramu 11

Bezaleli

Hili ni jina la mwanaume.

Exodus 38:30

Maelezo ya Jumla

Bazaleli na kundi lake wanaendelea kujenga maskani na vifaa.

kiunzi

Hii ni fremu ya chuma ya kushikilia mbao inapo chomwa.

Exodus 39

Exodus 39:1

Maelezo ya Jumla

Bezaleli na kundi lake wanaanza kutengeneza mavazi ya kikuhani.

wakafanya

Neno "wakafanya" lina husu Bezaleli, Oholiabu, na wafanya kazi wingine.

kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa

"sawa na Yahweh alivyo mwambia Musa kufanya"

Exodus 39:2

Maelezo ya Jumla

Bazaleli na kundi lake wanaendelea kutengeneza mavazi ya kikuhani.

Bezaleli

Hili ni jina la mwanaume.

Exodus 39:4

Maelezo ya Jumla

Bazaleli na kundi lake wanaendelea kutengeneza mavazi ya kikuhani.

ulikuwa wa kitambaa kilekile, kitani bora kilichosokotwa

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

kama vile Yahweh alivyokuwa amemwamuru Musa

"sawa na Yahweh alivyo mwambia Musa kufanya"

Exodus 39:6

Maelezo ya Jumla

Bazaleli na kundi lake wanaendelea kutengeneza mavazi ya kikuhani.

muhuri

Hili lilikuwa jiwe lilochorwa ambalo lilitumika kutia alama ya mchoro kwenye kitambaa kibichi.

kama vile Yehova alivyokuwa amemwamuru Musa

"sawa na Yahweh alivyo mwambia Musa kufanya"

Exodus 39:8

Maelezo ya Jumla

Bazaleli na kundi lake wanaendelea kutengeneza mavazi ya kikuhani.

Kisha akafanya

"Bezaleli akafanya" au "Bezaleli na wafanya kazi wakafanya"

shubiri

Shubiir ni sentimita 23.

Exodus 39:10

Maelezo ya Jumla

Bazaleli na kundi lake wanaendelea kutengeneza mavazi ya kikuhani.

Kisha wakakijaza

"Wafanya kazi wakaweka kwenye mshipi"

zabarijadi ... yaspi

Baadhi ya lugha zinaweza zisiwe na maneno ya baadhi ya haya mawe. Kitu cha muhimu ni kwamba yalikuwa na dhamani na yalitofautiana.

Yaliwekwa katika mapambo ya dhahabu

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 39:14

Maelezo ya Jumla

Bazaleli na kundi lake wanaendelea kutengeneza mavazi ya kikuhani.

Na mawe hayo yalikuwa kulingana

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 39:17

Maelezo ya Jumla

Bazaleli na kundi lake wanaendelea kutengeneza mavazi ya kikuhani.

kamba mbili

"kamba zilizo tengenezwa kwa dhahabu safi na kusokotwa kama waya"

Exodus 39:19

Maelezo ya Jumla

Bazaleli na kundi lake wanaendelea kutengeneza mavazi ya kikuhani.

mshipi

Hii ilikuwa nguo iliyo tengenezwa kwa nyuzi mtu aliyo sokotwa pamoja kufanya uzi mgumu.

Exodus 39:21

Maelezo ya Jumla

Bazaleli na kundi lake wanaendelea kutengeneza mavazi ya kikuhani.

ili kipate kuwa juu ya

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

kifuko cha kifuani kisiondoke juu ya efodi

"kifuko cha kifuani kitabaki kwenye efodi"

Exodus 39:22

Maelezo ya Jumla

Bazaleli na kundi lake wanaendelea kutengeneza mavazi ya kikuhani.

Bezaleli

Hili ni jina la mwanaume.

Exodus 39:25

Maelezo ya Jumla

Bazaleli na kundi lake wanaendelea kutengeneza mavazi ya kikuhani.

kengele za dhahabu safi

Hizi zilikuwa kengele ndogo.

kengele na komamanga, kengele na komamanga

Hivi ndivyo mfumo una paswa kurudiwa chini ya pindo la joho.

Exodus 39:27

Maelezo ya Jumla

Bazaleli na kundi lake wanaendelea kutengeneza mavazi ya kikuhani.

Kisha wakafanya ... amemwamuru Musa

Kwa 39:27-29 ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno katika 28:39 na 28:40 na 28:42

kilemba

Hichi ni kifuniko cha kichwa kinacho valiwa na wanaume kilicho tengenezwa na mistari mirefu ya kitambaa.

ukumbuu

Hichi ni kitambaa kirefu kinacho valiwa mabegani au kufungwa kiunoni.

Exodus 39:30

Maelezo ya Jumla

Bazaleli na kundi lake wanaendelea kutengeneza mavazi ya kikuhani.

ishara takatifu

Hichi kilikuwa ni taji lilo wafanya kwa dhahabu safi.

Exodus 39:32

Maelezo ya Jumla

Waisraeli wana maliza kufanya vitu Yahweh alivyo waamuru katika 35:4 na 35:10

Basi kazi ya ile maskani ya hema la mkutano ikafikia mwisho wake. Kwa maana wana wa Israeli waliendelea kufanya kulingana na yote

"Maskani" na "hema la kukutani" ni kitu kimoja. Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

viunzi

Vifungo vinatoshea kwenye tanzi ili kushikilia pazia pamoja.

Exodus 39:36

Maelezo ya Jumla

Bezaleli na kundi lake wanaendelea kuonyesha yote waliyo mtengenezea Musa.

mkate wa wonyesho

Huu mkate uliwakilisha uwepo wa Mungu.

kiunzi

Hii ni fremu ya chuma iliyo shikilia mbao wakati inapo waka.

Exodus 39:40

Maelezo ya Jumla

Bezaleli na kundi lake wanaendelea kuonyesha yote waliyo mtengenezea Musa.

Wakaleta

"Watu wa Israeli wakaleta"

maskani, kwa ajili ya hema ya kukutania

Hii ina maana ya kitu kimoja.

Exodus 39:42

Kulingana na yote

"Na kisha watu"

tazama

Neno "tazama" hapa linaleta umakini wa maelezo yanayo fuata.

kama vile Yahweh alivyokuwa ameamuru. Hivyo ndivyo walivyokuwa wamefanya.

Walifanya kama Yahweh alivyo waamuru"

Exodus 40

Exodus 40:1

Siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza ya mwaka

Mwaka mpya una hashiria wakati ambao Mungu aliwaokoa watu wake kutoka Misri. Hii inatokea wakati wa Machi kwa kalenda za Magharibi.

Exodus 40:3

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendela kumwambia Musa nini watu wafanye.

Utaweka sanduku la ushuhuda ndani yake

"weka sanduku la amri za agano katika kitunzi takatifu"

utaziba sanduku kwa pazia

"weka sanduku nyuma ya pazia"

Exodus 40:5

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendela kumwambia Musa nini watu wafanye.

sanduku la ushuhuda

Hii ya husu "kitunzi takatifu"

Exodus 40:8

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendela kumwambia Musa nini watu wafanye.

samani zake

"vitu vyote ambavyo ni sehemu yake"

Exodus 40:12

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa.

Umlete

Musa atafanya hivi vitu mwenyewe.

yaliyo tengwa kwa ajili yangu

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Exodus 40:14

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Musa

vizazi vyote vya watu wao

"katika vizazi vyote vya uzao wao"

Exodus 40:17

Hivyo hema la kukutania liliandaliwa

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

siku ya kwanza ya mwezi

Mwaka mpya una hashiria wakati ambao Mungu aliwaokoa watu wake kutoka Misri. Hii inatokea wakati wa Machi kwa kalenda za Magharibi.

mwaka wa pili

Huu ni mwaka wa pili Yahweh alipo watoa watu wake Misri.

Musa alianda

Musa alikuwa kiongozi. Watu walisaidia kuandaa maskani.

nguzo

kipande kigumu cha mbao kilicho nyooshwa wima kusaidia

Exodus 40:21

Aliichukuwa

Musa alikuwa kiongozi. Alikuwa na wafanya kazi wakimsaidia

ili lizibe

"mbele ya"

Exodus 40:24

Alieka kinara cha taa kwenye hema la kukutania

Musa aliwaelekeza kusogeza kinara. Hii yaweza andikwa kwa wazi katika tafsiri.

Exodus 40:26

mbele ya pazia

Hili pazia lilitenganisha sehemu takatifu kutoka sehemu takatifu sana. Hii yaweza andikwa wazi katika tafsiri.

Exodus 40:31

waliosha mikono yao na miguu kwenye beseni

Waliosha na maji kutoka kwenye beseni.

Katika hili

"Na kisha"

Exodus 40:34

tukufu wa Yahweh ukafunika

"Uwepo mzuri wa Yahweh ukafunika"

Exodus 40:36

lilipo chukuliwa juu kutoka

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

lilipo nyanyuliwa juu

Hii yaweza andikwa katika tensi tendaji.

Leviticus 1

Leviticus 1:1

Yahweh

Hili ndilo jina la Mungu ambalo alilifunua kwa watu wake katika Agano la Kale.

kutoka kweye hema la kukutania, akisema, "Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, 'Mtu yeyote

Hapa Yahweh anaanza kuzungumza na Musa. Hotuba hii inamalizikia katika 3:17. Hii inaweza kufasiriwa bila nukuu ndani ya nukuu. :"Kutoka kwenye hema la kukutania na akamwambia Musa kuzungumza na watu wa Israeli: 'Mtu yeyote aletapo"

'Mtu yeyote kutoka miongoni mwenu

"mmoja wenu yeyote" au "yeyote wa kwenu"

Leviticus 1:3

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendele kumwambia Musa yawapasayo watu wa Israeli kufsny ili kwa mba sadaka zao zitakuwa zenye kubalika kwa Yahweh.

.Iwapo toleo lake ... naye itambidi kutoa

Hapa "yake" na "naye" humaanisha mtu aletaye sadaka kwa Yahweh. laweza kufasiriwa katika nafsi ya pili kama lilivyo katika 1:1 : iwapo toleo lako...yapasa utoe

ili iweze kukubalika mbele za Yahweh

Hili linaweza kufasiriwa katika muundo tendaji: :Ili kwamba Yahweh aikubali"

Ataweka mikono yake

Hiki ni kitendo cha kiishara kinachomfananisha mtu na mnyama anayemtoa. Katika njia hii mtu anajitoa mwenyewe kwa Yahweh kwa kupitia mnyama, ili kwamba Mungu atasamehe dahambi za mtu huyo wanapomuua mnyama.

ndipo itakuwa imekubalika badala yake ili kufanya upatanisho kwa ajili yake mwenyewe

Hii inaweza kufasiriwa katika muundo tendaji: "Kisha Yahweh ataikubali machini pake na kuzisamehe dhambi zake"

Leviticus 1:5

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa watu wanachotakiwa kufanya.

Naye yampasa kumchinja huyo fahali

Hapa "naye" humaanisha yule anayetoa hiyo sadaka. linaweza kutamkwa katika nafsi ya pili. : "Nawe yakupasa kumchinja huyo fahali"

mbele za Yahweh

"Katika uwepo wa Yahweh"

wataileta hiyo damu

Inadokeza kwamba makuhani wangeikinga damu kwenye bakuli ilipotiririka kutoka kwa mnyama. Kisha wangelileta hillo bakuli lenye damu ndani yake na kuliwasilisha kwaYahweh kwenye madhabahu.

Kisha ataichuna ngozi hiyo sadaka ya kuteketezwa na kuikatakata vipande.

Kama ilivyoonyeshwa kwenye 1:9, Mtu alilazimiika pia kuosha matumbo na miguu ya mnyama kwenye maji. Mhisika mwenyewe alilazimika kufanya hivyo kabla hajawapa makuhani vile vipande ili kwamba wangeweza kuviweka juu ya madhabahu. Unaweza kuyatamka hayo maelekeza kuwa yalikuwa ni matumbo na miguu.

Naye ataichuna ngozi

Hapa neno "naye" humaanisha yule anayetoa hiyo sadaka.

Leviticus 1:7

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa kiwapasacho watu kutenda ili matoleo yatakubalika kwa kwake.

wataweka moto juu ya madhabahu na kuweka kuni ili kuuchochea huo moto

Hili laweza kumaanisha kwamba makuhani mkaa wa moto juu ya madhabahu, kisha wakaweka kuni juu ya mkaa. : wataweka kunu juu ya madhabahu na kuwasha moto"

kuuchochea huo moto

Hii ni nahau inayomaanisha kuendelea kuweka kuni kwenye moto. Moto juu ya madhabahu nilazima uendelee kuwaka bila kuzimika

Lakini matumbo yake na miguu ataiosha kwa maji

Mtu huyo angefanya hivi kabla hajavitoa vipande kwa makuhani waviweke juu moto. U naweza kutamka hivi mwishoni mwa 1:5

Mtumbo

Ni hilo tumbo na utumbo

naye ataiosha

Hapa neno "naye" humaanisha anayetoa hiyo sadaka.

nayo italeta harufu ya kupendeza kwangu

Yahweh akiwa amependezwa na utoaji dhabihu wa dhati wa aabuduye unamezungumziwa kana kwamba Yahweh alikuwa amependezwa na harufu nzuri ya dhabihu.

sadaka iliyofanywa kwangu kwa moto.

Yahweh anamwambia Musa kwamba ni lazima matoleo yawe yanachomwa kwa moto. Hili laweza kutamkwa katika muundo tendaji. : "sadaka ya kuteketezwa kwangu"

Leviticus 1:10

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa liwapasalo watu kutenda

mbele za Yahweh

"katika uwepo wa Yahweh"

Leviticus 1:12

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa liwapasalo watu kutenda

Naye ataikata...iliyofanywa Kwake kwa moto.

Ajili ya 1:12-13, tazama 1:7 ili uone wingi wa maneno haya yalivyofasiriwa

Naye ataikata

Hapa neno "naye" humaanisha mtu anayetoa dhabihu. Laweza kufasiriwa katika nafsi ya pili. :"Nawe utaikata"

italeta harufu ya kupendeza kwa Yahweh

Yahweh akiwa amependezwa na utoaji dhabihu wa dhati wa aabuduye unamezungumziwa kana kwamba Yahweh alikuwa amependezwa na harufu nzuri ya dhabihu.

itakuwa sadaka ya iliyofanywa...kwa moto.

Yahweh anamwambia Musa kwamba ni lazima makuhani wazichome sadaka zao kwa moto. Sentensi hii inaweza kufasiriwa kwenye muundo tendaji. :"itakuwa sadaka ya kuteketezwa kwangu" au "itakuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Yahweh"

Leviticus 1:14

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa kiwapasacho watu kutenda

nyonga shingo na kukinyoa kichwa chake,

popotoa/songonyoa kichwa chake na kuking'oa kutoka mwilini

Kisha damu yake itachuruzishwa

Sentensi hii yaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji: "Kisha itampasa kuhani kuichuruzisha damu yake"

Leviticus 1:16

Ni lazima akiondoe

"Ni lazima kuhani"

kibofu chake pamoja na uchafu wake

Kibofu ni kwenye koromeo la ndege mahali ambapo chakula ambacho hakijameng'enywa hutunzwa.

nacho atakitupa...kando ya madhabahu

Neno "nacho" hapa humaanisha kibofu pamoja na uchafu wake

italeta harufu ya kupendeza kwa Yahweh

Yahweh akiwa amependezwa na utoaji dhabihu wa dhati wa aabuduye unazungumziwa kana kwamba Yahweh alikuwa amependezwa na harufu nzuri ya dhabihu. Tazama lilivyotafsiriwa hili katika 1:7

nayo itakuwa sadaka iliyofanywa Kwake kwa moto.

Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "itakuwa sadaka ya kuteketezwa kwangu" au "itakuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Yahweh"

Leviticus 2

Leviticus 2:1

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kumbia Musa liwapasalo watu kutenda.

liwe unga safi

"Iiwe unga safi kabisa" au "uwe unga uliobora"

unga

ngano ilinyosagwa

Itampasa kuipeleka

itampasa kuuchukua

atatwaa konzi

"atachukua unga anaoweza kuubeba mkononi mwake

sadaka ya kuwakilisha

konzi ya sadaka ya nafaka huwakilisha sadakanzima ya nafaka. Hii inamaanisha kwamba sadaka nzima ni ya Mungu.

Nayo itatoa harufu nzuri ya kupendeza kwa Yahweh.

Yahweh akiwa amependezwa na utoaji dhabihu wa dhati wa aabuduye unazungumziwa kana kwamba Yahweh alikuwa amependezwa na harufu nzuri ya dhabihu. Tazama lilivyotafsiriwa katika 1:7

Ni kitakatifu sana kwa Yahweh kutoka kwenye sadaka iliyofanywe kwa Yahweh kwa moto.

Hili laweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. : "itakuwa sadaka ya kuteketezwa Kwake"

Leviticus 2:4

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa kwamba watu hao pamoja na makuhani yawapasa wafanye hivyo ili sadaka zao ziweze kukubalika kwake.

uliookwa kweye tanuru

Sentensi hii yaweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "uliouoka kwenye tanuru"

tanuru

Huenda hiki kilikuwa ni chombo kilichotengenezwa kwa udongo chenye uwazi shimo katikati. Moto uliwashwa chini ya tanuru, na joto lingeoka donge la unga ndani ya tanuru.

mkate laini wa unga safi

yaeleweka kwamba mkate laini haukuwa na hamira.

uliopakwa mafuta

Tafsiri kirai hiki kuonesha kwamba mafuta ni lazima yapakwe kwenye mkate. :"pamoja na mafuta juu ya mkate"

Iwapo toleo lako la nafaka limeokwa kwa kikaango cha chuma

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : Iwapo unaioka sadaka yako ya nafaka katika kiaango cha chuma"

kikaango cha chuma

Hii ni sahani nzito iliyotengenezwa ama kwa udongo au chuma. Sahani iliwekwa juu ya moto, na donge la ungu lilipikwa juu ya sahani.

Leviticus 2:6

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia musa kwamba watu hao na makuhani yawapasa wafanye hivyo ili sadaka zao ziweze kukubalika kwake

utaigawanya

Hapa "inayogawanywa" ni sadaka ya nafaka iliyopikwa kwenye kikaaongo cha chuma.

Iwapo sadaka yako ya nafaka imepikwa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Ikiwa unaipika sadaka yako ya nafaka"

katika sufuria

Sufuria ilikuwa sahani yenye kingo zikiizunguka. Bonde la unga lilidumbuzwa ndani ya sufuria na kupikwa juu ya moto.

lazima iwe imeandaliwa

Yaweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Ni lazima uiandae"

Leviticus 2:8

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia musa kwamba watu hao na makuhani yawapasa wafanye hivyo ili sadaka zao ziweze kukubalika kwake

ililofanywa kwa vitu hivi

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. : "ulioutengeneza kutokana na unga na mafuta"

nayo itawasilishwa

Yaweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Utaiwasilisha"

Ndipo kuhani... ifanywayo kwa moto.

Kwa ajili ya2:9-10 tazama maelezo ya sura ya 2:1

sadaka ya kuwakilisha

Tazama maelezo ya sura ya 2:1

Itakuwa sadaka kuiliyofanywa kwa moto

Hii inaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. : "Itakuwa sadaka ya kuiteketeza"

italeta harufu ya kupendeza kwa Yahweh

Tazama maelezo ya sura 1:7

kutoka kwenye sadaka ifanywayo kwa Yahweh kwa moto

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. : "kutoka kwenye sadaka ya kuiteketeza kwa Yahweh"

Leviticus 2:11

Maelezo ya Jumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa kwamba watu hao na makuhani yawapasa wafanye hivyo ili sadaka zao ziweze kukubalika kwake

Hakutakuwa na sadaka ya nafaka utoayo kwa Yahweh itakayofanyizwa kwa hamira

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. : "Usitumie hamira kwenye sadaka ya nafaka uitoayo kwa Yahweh"

kuwa sadaka ifanywayo kwa moto

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. : "kuwa sadaka ya kuteketeza

Nawe utazitoa

"Nawe utazitoa sadaka za nafaka zilizo na hamira au asali"

hazitatumika kuleta harufu ya kupendeza itolewayo juu ya madhabahu

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. ; "utazitumia kuleta harufu ya kupendeaza juu ya madhabahu" au "hutaziteketeza juu ya madhabu"

chumvi ya agano la Mungu wako

Huashiria kwamba chumvi ni ishara inayowakilisha agano la Mungu.

Leviticus 2:14

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa kwamba watu hao na makuhani yawapasa wafanye hivyo ili sadaka zao ziweze kukubalika kwake

iliyobanikwa kenye moto, na kupondwa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. : "Ile uliyoipika kwenye moto na kisha kusagwa"

sadaka ya kuwakilisha

Tazama maelezo katika sura ya 2:1

Hii ni sadaka ifanywayo kwa Yahweh kwa moto.

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. : "Hii ni sadaka ya kutekezwa kwa Yahweh"

Leviticus 3

Leviticus 3:1

Taarifa kwa ujumla

Musa anaendelea kuwaambia watu kile ambacho Yahweh anataka wao wafanye.

mbele za Yahweh

"katika uwepo wa Yahweh" au "kwa Yahweh"

Ataweka mikono yake

Hili ni tendo la kiishara ambalo humfananisha mtu na mnyama anayemtoa. Katika njia hii mtu huyo anajitoa mwenyewe kwa Yahweh kwa kupitia mnyama. Tazama lilivyotafsiriwa katika sura ya 1:3

wana wa Aroni watainyunyiza damu yake

Inaashiria kwamba kabla hawajainyunyiza damu ,waliikinga kwanza hiyo damu katika bakuli walipokuwa akiichuruzisha kutoka kwa Munyama.

Leviticus 3:3

Matumbo

Hili ni tumbo na utumbo

ya kiununi

Hii ni sehemu ya mwili wa mnyama kwenye maeneo ya ndani ya uti wa mgongo kati ya mbavu na mfupa wa nyonga.

kitambi cha ini

Hii ni sehemu ya ini iliyojikunja au kulizunguka. Sehemu hii huonekana kuwa ni sehemu ya ini iliyobora kabisa kwa kula. : "Sehemu ya ini iliyobora"

Hii italeta harufu ya kupendeza mbele za Yahweh

Tazama ufafanuzi uliotolewa katika sura ya 1:7

itakuwa sadaka itolewayo Kwake kwa moto.

Hili laweza kutafsiriwa katika mtindo tendaji. : "nayo itakuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Yahweh"

Leviticus 3:6

amtoe mbele za Yahweh

"amtoe mkatika uwepo wa Yahweh" au "amte kwa Yahweh"

Ataweka mkono wake juu ya kichwa

Hili ni tendo la kiishara ambalo humfananisha mtu na mnyama anayemtoa. Kwa njia hii mtu huyo atakuwa anajitoa mwenyewe kwa Yahweh kupitia mnyama.

wana wa Aroni watanyunyiza damu

Inaashiria kwamba kabla hawajanyunyiza hiyo damu, waliikinga kwanza kwenye bakuli ilipokuwa inachuruzika kutoka kwa mnyama

Leviticus 3:9

sadaka ifanywayo kwa moto

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "kuwa sadaka ya kuteketezwa"

Yale mafuta, mafuta yote...na hizo figo —ataiondoa hii yote.

Lile tamko "ataiondoa hii yote" laweza kuwekwa mwanzoni mwa sentensi. : "Atayaondoa mafuta, hayo mafuta yote...hizo figo"

matumbo

Sehemu hizi ni tumbo na utumbo.

yaliyo karibu na matumbo, na figo zote mbili

Sentensi mpya yaweza kuanzia hapa. : "iliyo karibu na mbatumbo. Ni lazima ataziondoa hizo figo"

karibu na kiuno

Hii ni sehemu ya mwiili kwenye sehemu ndani ya uti kati ya mbavu na mfupa wa nyonga.

kitambi cha ini

Hii ni sehemu ya ini yenyekupinda au kulizunguka. Sehemu hii huonekana kuwa bora sana kwa kula. : "ile sehemu ya ini iliyobora kabisa"

ataiteketeza yote juu ya madhabahu kuwa sadaka ya chakula ya kuteketezwa kwa Yahweh

Hapa haikukusudiwa kumaanisha kwamba Yahweh hula chakula. : "ataviteketeza vitu hivyo juu ya madhabahu viwe sadaka kwa Yahweh. Vitu hivyo vitatokana na mazao yako ya chakula"

Leviticus 3:12

mbele za Yahweh

"katika uwepo wa Yahweh" au "kwa Yahweh"

Ataweka mikono yake juu ya kichw

Hili ni tendo la kiishara ambalo humfananisha mtu na mnyama anayemtoa. Kwa njia hii mtu huyo atakuwa anajitoa mwenyewe kwa Yahweh kupitia mnyama.Tazama maelezo katika 1:3

wana wa Aroni watainyunyiza damu yake

Inaashiria kwamba kabla hawajainyunyiza hiyo damu, waliikinga kwanza kwenye bakuli ilipokuwa ikichuruzika kutoka kwa mnyama.

atatoa dhabihu yake iliyofanywa kwa mot

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "ataitoa sdhabihu yake kwa moto" au "ataichoma dhabihu yake"

Leviticus 3:15

Naye ataziondoa pia

Neno "naye" hapa humaanisha mtu anayetoa dhabihu.

ataiteketeza hiyo yote juu ya madhabahu kuwa matoleo ya chakula ya kuteketezwa

Hapa haikukusudiwa kumaanisha kwamba Yahweh hula chakula. : "ataviteketeza vitu hivyo juu ya madhabahu viwe sadaka kwa Yahweh. Kitakuwa ni chakula chao alichopwa Yahweh"

kutoa harufu ya kupendeza

Yahweh hupendezwa na harufu ya nyama iliyochomwa anapopendezwa na usafi wa aabuduye. Tazama lilivyotafsiriwa katika 1:7

Itakuwa ni amri ya kudumu kwa vizazi vya watu wako

Hii humaanisha kwamba wao pamoja na vizazi vyao lazima waitii amri hii.

au damu

"au kutumia damu"

Leviticus 4

Leviticus 4:1

Yahweh akazungumza na Musa akisema, "Waambie watu wa Israeli, 'mtu yeyote atendapo dhambi

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Nukuu halisi yaweza kutamkwa kama nukuu taarifa iliyotajwa. : Yahweh akazungumza na Musa na akamwambia awaambie watu wa Israeli hivi: 'Mtu yeyote atendapo dhambi"

ambayo Yahweh ameagiza yasitendwe

Hili laweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. : "Ambayo Yahweh amewaamru watu wastende"

endapo anafanya jambo fulani lililokatazwa,

Hili laweza kufasriwa katika mtindo tendaji. : "iwapo anafanya jambo ambalo Yahweh aliruhusu"

yafuatayo lazima yafanyike

Hiii yaaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. : "yapasa afanye yafuatayo"

na kuleta hatia juu ya watu

Ile nomono dhahania "hatia" yaweza kutamkwa kama kivumishi. : "kwa kiasi cha kusababisha watu kujisikia wenye hatia"

Leviticus 4:4

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa kiwapasacho watu kutenda.

Atamleta huyo fahali

"Kuhani atamleta huyo fahali"

ataweka mikono yake juu ya kichwa chake

Tazama maelezo ya sura 1:3 uone lilifasiriwa.

Kuhani mpakwa mafuta atachukua sehemu ya damu

Inaonyesha kwamba kuhani aliikinga kwanza damu kwenye bakuli ilipokuwa inachuruzika kutoka kwa huyo mnyama.

Leviticus 4:6

kuinyunyiza

"kutiririsha sehemu yake" au "kudondosha sehemu yake"

pembe za madhabahu

hii humaanisha kwenye kona za madhabahu. Zimesongoka kama pembe za makisai. : "Michomozo iliyo kwenye kona za madhabahu"

ataimwaga chini

"ataitupa nje damu iliyobaki"

kwenye kitako cha madhabahu

chini ya madhabahu

Leviticus 4:8

Naye atayakata

"Kuhani atayakata"

yale mafuta yanayofunika matumbo. ..pamoja na figo—ataikata hii yote

Yale maelezo "ataikata hii yote" yaweza kuwekwa mwanzoni mwa sentensi. : "Atayakata mafuta yote yafunikayo matumbo...pamoja na hizo figo"

matumbo.

Haya ni tumbo na utumbo

karibu na kiuno

Hii ni sehemu ya mwili juu ya upande wa ndani wa uti wa mgongo kati ya mbavu na mfupa wa nyonga.

kitambi cha in

Hii ni sehemu ya ini iliyojikunja au kulizunguka. Sehemu hii huonekana kuwa ni sehemu ya ini iliyobora kabisa kwa kula. : "Sehemu ya ini iliyobora"

Leviticus 4:11

Ngozi ... mabaki yoyote ya nyama, atazipeleka hizo zote nje

Yale maelezo "atazipeleka hizi zote" Yaweza kuweka mwanzoni mwa sentensi. : "Kuhani atapeleka nje hiyo ngozi..mabaki ya fahali"

eneo ambalo wamelisafisha kwa ajili yangu

Eneo kuwa safi kiibada na pa kufaa kutumia katika kumtumikia Mungu linasemwa kuwa lilikuwa safi kimaumbile.

wamelisafisha kwa ajili yangu

"Wamelisafisha" hapa humaanisha hao makuhani na "Mimi" humaanisha Yahweh.

Leviticus 4:13

bila kukusudia

"bila kujua"

ameamru yasitendwe

Hili laweza kuutamkwa katika mtindo tendaji. : "alichowaamru wasikitende"

hiyo dhambi waliyoitenda ikawa imejulikana

Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "wanapotambua kwamba wametenda dhambi"

wataweka mikono yao juu ya kichwa

Tazama maelezo katika sura 1:3 uone lilivyofasiriwa

huyo fahali atachinjwa

Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Nao watamuua huyo fahali"

Leviticus 4:16

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Munsa yawapasayo watu kutenda.

Kuhani aliyepakwa mafuta ataleta damu

Inamaanisha kwamba huyo kuhani aliikinga damu kwenye bakuli ilipotiririka

mbele ya pazia.

Inamaanisha kwamba hili ni pazia mbele ya patakatifu pa patakatifu

Leviticus 4:18

Ataweka

"Naye kuhani ataweka"

pembe za madhabahu

hii hurejelea kona za madhabahu. Zimechongwa kama pembe za ng'ombe. Tazama lilivyofasiriwa katika Sura ya 4:6

ataimwaga damu yote

Ataimwaga damu iliyosalia

mafuta yote kutoka kwake

"mafuta yote kutoka kwa mnyama na kuyachoma hayo mafuta"

Leviticus 4:20

inavyompasa kumfanyia

"Ni lazima kuhani afanye"

kuhani atawafanyia watu upatanisho

Nomino dhahania "upatanisho" yaweza kama kitenzi. : "Kuhani atapatanisha kwa ajili ya kwa ajili ya dhambi za watu"

nao watakuwa wamesahewa

Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Naye Yahweh atawasamehe wao"

Leviticus 4:22

Yahweh Mungu wake ameamru yasitendwe

hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Mungu amewaamru watu wasitenda"

Nayo dhambi yake aliyoitenda imefahamisha kwake

hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. ; "kisha naye ameshatambua kwamba katenda dhambi"

Leviticus 4:24

Naye ataweka

"Mtawala ataweka"

ataweka mkono wake juu ya kichwa

Tazama lilivyofassiriwa katika sura ya 1:3

mahali ambapo huchinja

"makuhani wanapochinja"

mbele za Yahweh

"katika uwepo wa Yahweh" au kwa Yahweh"

Kuhani ataichukua damu

Inamaanisha kwamba kuhani aliikinga damu kwenye bakuli damu ilipotirirka kutoka kwa mbuzi.

pembe za madhabahu

Tazama maelezo kwenye sura ya 4:6 uone linavyofasiriwa

Leviticus 4:26

Naye atateketeza

"Kuhani atateketeza

Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya mtawala

Ile nomino dhahania "upatanisho"yaweza kutaamkwa kama kitenzi. : "Kuhani atapatanisha kwa ajili ya mtawala"

naye mtawala kulingana

Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Yahweh atasamehe dhambi za mtawala"

Leviticus 4:27

Yahweh amemwamru yeye yasitendwe

Watu wote wa Israeli waliamriwa wasitende dhambi. Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Yahweh aliwaamru watu wasiyatende"

dhambi yake aliyoitenda itakuwa imejulikana kwake

Hili laweza kutmkwa katika mtindo tendaji. : "naye amekuwa na ufahamu juu ya dhambi aliyoitenda.

Leviticus 4:29

Ataweka mkono wake juu ya kichwa

Tazama mafafanuzi katika sura ya 1:3 uone lilivyofasiriwa

Kuhani atachukua kiasi cha damu

Inamaanisha kwamba kuhani aliikinga damu ya kwenye bakuli wakati ilipotiririka kutoka kwa mnyama

pembe za madhabahu

Tazama katika sura ya 4:6 uone lilivyofasiriwa.

Damu yote iliyobaki

Damu yote iliyobaki kwenye bakuli.

Leviticus 4:31

Naye atayakata

"Naye'" hapa humaanisha yule mtu anayetoa sadaka

yanvyokatwa hayo mafuta

Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "ni kama tu vile mtu akatavyo hayo mafuta"

ataiteketeza

"atayachoma mafuta"

ili kuleta harufu ya kupendeza kwa Yahweh

Tazama maelezo yaliyotolewa kwenye sura 1:7 ili uone maneno hayo yalivyofafanuliwa

Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya mtu hyo

Ile nomino dhahania "upatanisho" yaweza kutamkwa kama kitenzi. "Kuhani atapatanisha kwa ajili ya dhambi za mtu huyo"

naye atakuwa amesamehewa.

Hili laweza kutamkwa katika mtingo tendaji. : "Yahweh atazisamehe dhambi za mtu huyo"

Leviticus 4:32

Ataweka mkono juu ya kichwa

Tazama maelezo ya sura ya 1:3 ili kuona lilivyofasiriwa.

mahali wanapochinja s

"mahali makuhani wachinjapo"

Leviticus 4:34

pembe za madhabahu

Tazama maelezo ya sura ya 4:6 ili kuona linavyofasiriwa.

naye ataimwaga damu yake yote

"Naye ataimwaga damu yake yote iliyobaki"

Naye tayakata mafuta

"Naye" hapa humrejelea mtu anayetoa hiyo dhabihu.

kama tu vile yakatwavyo mafuta ya mwana-kondoo

Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "kama tu vile mtu akatavyo hayo mafuta ya Mwana-kondoo"

matoleo ya Yahweh yafanywayo kwa moto

Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Matoleo ya kuteketezwa kwa Yahweh

atafanya upatanisho kwa ajili yake kwa dhambi aliyoifanya

Ile nomino dhahania "upatanisho" yaweza kutamkwa kama kitenzi. :atapatanisha kwa ajili ya dhambi aliyotenda huyo mtu"

na mtu huyo atakuwa amesahewa.

Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Yahweh atasameha dhambi ya mtu huyo"

Leviticus 5

Leviticus 5:1

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendlea kumwambia Musa yawapasayo watu kutenda

ushahidi fulani kuhusu kile alichotakiwa kushudia

Sheria na viongozi wa kiyahudi viliwataka watu kushuhudia iwapo walikuwa mashahidi kwa uharifu. Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "jambo fulani ambalo hakimu amemtaka yeye kushuhudia"

Mungu amekitaja kuwa ni najisi

Kitu fulani ambacho Mungu amekita kuwa hakiwafai watu kukigusa au kukila kimesemwa kuwa kana kwamba kilikuwa kichafu kwa mwonekano.

mzoga

"maiti"

yeye ni najisi

Mtu asiyekubalika katika makusudi ya Munngu husemwa kana kwamba ni mtu aliyekuwa mchafu kimwili.

Leviticus 5:3

ikiwa agusa unajisi wa mtu fulani, haijalishi ni unajisi wa aina gani

Ile nomino dhahania "unajisi" yaweza kutamkwa kama kivumishi. : "iwapo nagusa kitu chochote ambacho humfanya mtu najisi"

unajisi

Kitu fulani ambacho Yahweh amekitamka kuwa hkifai kwa mtu kukigusa au kukila huzungumziwa kana kwamba kilikuwa najisi kwa monekao.

hakuwa na habari juu yake

"yeye ahitambui" au "hajui juu yake"

anaapa kwa midomo yake

Hapa "midomo" huwakilisha mtu mzima. : "iwapo mtu yeyote anaapa bila kujali"

mtu huapa bila kujali,

Hii humaanisha kuapa kiapo bila kufikiri kwa kumaanisha juu yake. Inamaanisha kwamba baada ya mtu kuwa anaapa kiapo ambacho ama hawezi kukitimiza au hataki hasa kukitimiza.

Leviticus 5:5

Maelezo kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa yawapasayo watu kutenda.

naye kuhani atafanya upatanisho

Ile nomino dhahania "Upatanisho" yaweza kutamkwa kama kitenzi. : "Kuhani atapatanisha kwa ajili yake"

Leviticus 5:7

Iwapo hataweza kununua mwana-kondoo

Iwapo hana fedha ya kutosha kununua mwana-kondoo

naye atamvunja shingo yake lakini ataacha kichwa chake kinaning'inia wala hataiondoa kabisa shingo yake

"naye atamuua kwa kukipindua kichwa chake na kuivunja shingo yake, lakini hatakiondoa hichwa"

Leviticus 5:10

kama ilivyoelezwa kwenye maelekezo

Hii yaweza kutakwa katika mtindo tendaji. : "kama alivyoelekeza Yhweh"

naye kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya dhambi aliyotenda

Ile nomino dhahania "upatanisho" yaweza kutamkwa kama kitenzi. : "Naye kuhani atapatanisha kwa ajili ya dhambi ile ambayo ametenda

naye huyo mtu atakuwa amesamehewa

Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Yahweh atamsamehe mtu huyo"

Leviticus 5:11

sehemu ya kumi ya efa

Efa moja ni sawa sawa na lita 22. Sehemu ya kumi ni kama lita 2 hivi

sehemu ya kumi

Hii ni sehemu moja ya kumi zilizo sawa

Leviticus 5:12

Naye atauleta

"Naye yampasa kuleta unga safi"

sadaka ya kuwakilisha

konzi kuhani chomayo juu ya madhabahu huwakakilisha matoleo yote. Hii humaanisha matoleo yote ni ya Yahweh, tazama sura ya 2:1

atafanya upatanisho

Ile nomino dhahania "upatanisho" yaweza kutamkwa kama tendo. : "atamatanisha"

juu ya madhabahu, na juu ya matoleo yafanywayo kwa Yahweh

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : " Yahweh. : "juu ya sadaka za kuteketezwa kwa Yahweh"

naye mtu huyo atakuwa amesahewa.

Hili laweza kutamkwa kama mtindo tendaji. : "Yahweh atasamehe dhambi za mtu huyo"

Leviticus 5:14

dhambi dhidi ya vitu ambavyo ni vya Yahweh

Hii inamaanisha kwamba mtu aliyefanya dhambi kwa kutotoa kwa Yahweh kile alichomwamru Yahweh kutoa. : "Natenda dhambi kwa kushindwa kutoa kwa Yahweh kilicho cha Yahweh"

thamani yake halisi itatathminiwa kulingana na shekeli za fedha

Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji: "Naye yapasa kuamua ni shekeli ngapi huyo kondoo dume anastahili"

shekeli

Sheli ni kama gramu 11 hivi katika uzito.

shekeli za patakatifu

Labda huenda hii humaanisha kulikuwa angalau na njia mbili za kupima shekeli. Hii humaanisha namna kuhani wa patakatifu alivyopima shekeli. : ""kipimo rasimi katika hema takatifu"

patakatifu

Hili ni jina lingine la hema takatifu

ataongeza moja ya tano

ya tano - Hii inamaanisha mtu huyo alilazimika kulipa ziada ya moja ya tano ya thamani ya alichodaiwa na Yahweh.

moja ya tano

ya tano - Hii ni sehemu moja kutokana na sehemu tano zilizosawa.

Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake

Ile nomino dhahania "upatanisho" yaweza kutamkwa kama kitenzi. "kuhani atapatanisha kwa ajili yake"

naye mtu huyo atakuwa amesamehewa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "yahweh atamsamehe mtu huyo"

Leviticus 5:17

ameagiza lisitendwe

Hii yaweza kutakwa katika mtindo tendaji. : ": "amewaamuru watu wasitende

atachukua hatia yake mwenyewe

Ile hatia ya mtu imezungumziwa kana kwamba ni kitu kinachoonekana ambacho mtu hukibeba. Neno "hatia" hapa huwakilisha kwa hatia hiyo. : "naye anawajibika kwa hatia yake mwenyewe" au "Yahweh atamwadhibu yeye kwa dhambi zake"

mwenye thamani ya fedha iliyopo

Hii humaanisha kuwa mtu huyo ni lazima aamue kwa kutumia kipimo rasimi cha kwenye hema takatifu ni kiasi gani cha shekeli huyo kondoo dume anastahili.

naye atakuwa amesamehewa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Yahweh atamsamehe yeye"

na kwa hakika amekuwa na hatia mbele za Yahweh."

"Hakika Yahweh ataiangalia hatia yake"

Leviticus 6

Leviticus 6:1

kuvunja amri dhidi ya Yahweh

"aasiye mojawapo ya amri za Mungu"

kujishughulisha na uongo dhidi ya jirani yake kuhusu kitu fulani kilichowekwa amana kwake

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. : "akidanganya kwa jirani yake kuhusu kitu fulani alichomwazimisha yeye

jirani yake

"Jirani yake" humaanisha Mwisraeli yeyote, siyo yeyote aishiye karibu naye.

alichokichukua kwa dhuluma kutoka kwake

Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "bila kurudisha kitu fulani alichokiazima"

Leviticus 6:5

kwa ukamilifu

"kikamilifu" au "kabisa"

kuongeza moja ya tano

Tazama lilivyotafsiriwa katika 5:15

kumlipa anayedai

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. :"kulipa mtu anayemdai"

anayopatikana na hatia

Mtu aliyeiba yapasa kuletwa mbele ya mwamuzi na kutangazwa mwanyehatia. : "sentensi hii yaweza kutamkwa katika mtindo tendaji. "hakimu anamtangaza kuwa mwenye hatia"

inayolinga na thamani ya sasa

Tazama 5:14 uone lilivyofasiriwa

Naye kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yake

Ile nomino dhahania "upatanisho" yaweza kutamkwa kama kitenzi. : "kuhani atapatanisha kwa ajili yake"

mbele ya Yahweh,

katika uwepo wa Yahweh"

naye atakuwa amesamehewa

Hii humaanisha Yahweh atamsamehe mtu huyo, siyo kuhani. Hii yaweza kutafasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Mungu atamsamehe yeye"

Leviticus 6:8

Kisha Yahweh akazungumza na Musa akisema, "Mwagize Aroni na wanawe, kusema, 'hii ndiyo sheria

Hii ina nukuu ndani ya nukuu. nukuu ya moja kwa moja yaweza kutamkwa kama nukuu taarifa yenyekutajwa. : "Kisha Yahweh akazungumza na Musa na kumwambia kumwamru Aroni na wanawe, akisema, 'Hii ndiyo sheria'"

juu ya meko ya madhabahu

"Lazima iwe juu ya madhabahu"

nao moto wa madhabahu utaendelea kuwaka.

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yapasa uufanye moto wa madhabuni uendelee kuwaka"

Leviticus 6:10

nguo zake za kitani,

Kitani ni nguo nyeupe. : "nguo zake nyeupe"

Naye atayachukua hayo majivu

"Naye atayakusanya hayo majivu"

baada ya moto kuwa umetekeza sadaka ya kuteketezwa

Moto kuteketeza kabisa sadaka umezunguzwa kana kwamba umeitafuna au kuitumia sadaka ya kutekezwa

mpaka mahali palipo safi

Mahali panapofaa kutumika kwa makusudi ya Mungu pameongelewa kana kwamba palikuwa safi kimaumbile.

Leviticus 6:12

Huo moto ulio juu ya madhabahu utaendelea kuwaka.

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Kuhani atautunza moto ulio juu ya madhabahu ili uendelee kuwaka"

kama inavyotakiwa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "juu yake kama Yahweh anavyotaka"

Leviticus 6:14

kuleta harufu ya kupendeza

Tazama sura 1:7 lilivyofasiriwa kama kirai kile kile.

sadaka ya kuwakilisha

Tazama lilivyotafsiriwa sura ya 2:1

Leviticus 6:16

ni lazima iliwe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. : "Yawapasa kuila"

Haitaokwa pamoja na hamira

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "msiioke na hamira"

matoleo... yafanywayo kwa moto

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "sadaka za kuteketeza"

Yeyote ayagusaye atakuwa mtakatifu."

Hili ni onyo limaanishalo kwamba hao walio wa uzao wa Aroni wasio wanaume haikuwapasa kuigusa hiyo sadaka. Maana kamili ya kauli hii yaweza kuwa wazi.

Leviticus 6:19

ambayo kila mwana atapakwa mafuta

hii inamaanisha kwamba watapakwa mafuta watakapokuwa makuhani. Maana ya kamili ya kauli yaweza kuwekwa wazi. Hii pia yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Anapompaka mafuta kila mwana, akiwaweka wakfu kuwa makuhani"

sehemu ya kumi ya efa

Efa moja ni sawasawa na lita 22. moja ya kumi ya efa ni kama lita 2 hivi.

sehemu ya kumi

Hii ni sehemu ya kumi sehemu zilizosawa.

Leviticus 6:21

Nayo Itatengenezwa

hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Nawe utaitengeneza"

katika kikaango

Tazama sura ya 2:4 uone lilivyofasiriwa.

Itakapokuwa imelowekwa

"Unga unapokuwa umeloana kabisa kwa mafuta"

utaileta ndani

Hapa "Nawe" humrejelea mtu anayetoa sadaka.

ili kuleta harufu ya kupendeza kwa Yahweh

Tazama maelezo katika sura ya 1:7 kwa ufafanuzi.

Kama ilivyoamriwa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Kama vile ambayo Yahweh amekuamru"

yote itateketezwa

Hii yaweza kutakwa katika mtindo tendaji. : "yapasa aiteketeze yote"

itateketezwa yote kabisa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo tendaji. : "Yapasa aiteketeze yote kabisa"

Haitaliwa kamwe

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Hakuna apaswaye kuila"

Leviticus 6:24

Yahweh akazungumza tena na Musa, akisema, "Sema na Aroni na wanawe uwaambie kwamba, 'Hii ndiyo sheria

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Nukuu ya moja kwa moja yaweza kutamkwa kama nukuu taarifa yenyekutajwa. : "Yahweh alizungumza na Musa na akamwambia kuzungumza na Aroni na wanawe, akimwambia, 'Hii ndiyo sheria'"

Sema na Aroni na wanawe

Yahweh anazungumza na Aroni na wanawe, lakini kanuni hizi zinatekelezeka kwa makuhani. Maana kamili ya maelezo haya yaweza kufanywa wazi.

Sadaka ya dhambi lazima ichinjwe... mbele za Yahweh

Yaweza kuwekwa wazi kwamba hii hurejelea upande wa kaskazini wa madhabahu. Tazama 1:10

inapochinjwa sadaka ya kuteketezwa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji:. : "Yakupasa kuichinjwa sadaka"

Sadaka ya dhambi lazima ichinjwe

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "mahali unapomchinjia mnyama wa sadaka ya kuteketezwa"

mbele za Yahweh

"kwa Yahweh"

Nayo yapasa kuliwa

Hii yaweza kutmkwa katika mtindo wa utendaji. : "Yampasa kuila"

Leviticus 6:27

Chochot kigusacho nyama yake kitakuwa kitakatifu

Hili ni onyo linalomaanisha kwamba zaidi ya makuhani hakuna impasaye kugusa nyama ya sadaka ya dhambi. Maana kamili ya maelezo haya yaweza kuweka wazi.

kama damu yake inanyunyizwa juu

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo tendaji. : "iwapo damu yake inanyunyizwa juu"

chungu ambamo inachemshiwa lazima kivunjwe

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "yakupasa kukivunja chungu ambacho ndani yake uliichemshia"

kama imechemshwa ndani ya chombo cha shaba, lazima kisuguliwe na kusafishwa kwa maji

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "kama ulichemsha nyama kwenye kwenye sufuria ya shaba, hivyo itakupasa kuisugua sufuria na kuisuuza kwa maji safi"

Leviticus 6:29

sadaka ya dhambi...haitaliwa

Hii yaweza kutamkwa ktika mtindo wa utendaji. "Hakuna hata mmoja atakayeila sadaka ya dhambi"

ambayo damu yake inaletwa kwenye hema la kukutania

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. ; Amabayo kutoka kwayo kuhanai anatoa damu ya kuleta kwenye hema la kukutania"

Ni lazima iteketezwe.

Hii yaweza kutamkwa ktika mtindo wa utendaji. : "lazima Kuhani ataiteketeza"

Leviticus 7

Leviticus 7:1

Taarifa kwa Ujumla:

Yahweh anaendelea kumwambia Munsa kile anachopaswa kumwambia Aroni na wanawe.

mahali panapostali kuchinjwa

Panaweza kuwekwa wazi kwamba hapa panamaanisha Mahali ambapo wanyama watolewao kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa huchinjwa. Tazama 1:10

Mafuta yote yaliyomo ndani yake yatatolewa:

Hii yaweza kufasiriwa katika mtido wa utendaji. : "Yule kuhani atayatoa mafuta yote yaliyomo ndani yake"

sehamu za ndani

Hili ni tumbo pamoja na Matumbo

Ini...figo

maneno haya yamefasiriwa katika mtindo ule ule uliotumika kwenye sura ya 3:3

karibu na kiuno

Hii ni sehemu ya mwili kwenye pande za uti wa mgonngo kati ya mbavu na mifupa ya nyonga. Tazama 3:3

hii yote lazima iondolewe

Hili linaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : Huyo Kuhani aiondoa hii yote.

Leviticus 7:5

viwe dhabihu iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "viwe sadaka ya kuteketezwa"

lazima iliwe

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Ni lazima waile"

Leviticus 7:7

Ni sheria ileile hutumika kwa zote mbili

"Sheria ni ileile kwa zote mbili"

ya kuhani azitumiaye kufanya upatanisho.

Ile nomino dhahania "Upatanisho" yaweza kutamkwa kama kitenzi. : "kwa kuhani aitoaye dhabihu ili kupatanisha kwa aji;li ya dhambi za mtu fulani"

ngozi

Vazi au ngozo ya mnyama

Leviticus 7:9

inayookwa mekoni... ipikwayo kaangoni

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Ile ambayo mtufulani anaioka mekoni... ile ambayo mtu fulani huipika mekoni"

Meko

Tazama maelezo katika sura 2:3

Kaango

Tazama maelezo katika 2:6 ili uone neno "kaango" lilivyotafsiriwa

Sufuria

Tazama sura ya 2:4 uone neno "sufuria" lilivyofasiriwa

Leviticus 7:11

mikate isiyotiwa hamira, bali iliyochanganywa na mafuta ya zeituni

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ya mikate aliyoifanya pasipo kutia hamira bali kwa kuchanganya na mafuta.

vipande vya mkate...iliyochanganywa na mafuta ya zeituni

"Vipande vya mkate" hapa humaanisha mkate mnene

kaki zisizotiwa hamira, lakini ziwe zimefanywa kwa mafuta ya zeituni yaliyopakwa juu yake

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji: : ya mikate miembamba aliyoifanya bila hamira bali kwa kuipaka mafuta"

kaki...zilizopakwa mafuta

"Kaki" hapa humaanisha mkate mwembamba.

mikate iliyofanywa kwa unga laini uliochanganywa vema na mafuta

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ya mikate aliyoitengeneza kwa unga laini uliochanganywa na mafuta"

mikate iliyofanywa kwa unga laini

"Mikate'" hapa humaanisha mkate mnene. Hufanana na aina ya ule mkate wa kwanza isipokuwa wenyewe unafanywa kwa unga uliolaini zaidi

Leviticus 7:13

vipande vya mikate iliyotiwa hamira

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji: : : "vipande vya mkate alioufanya kwa kutia hamira"

vipande vya mkate

Hii humaanisha mkate mnene.

Leviticus 7:15

Mtu anayeleta

"Mtu anayetoa"

kwa kusudi la kutoa shukrani

Ile nomino dhahania "shukurani" yaweza kutamkwa kama kitenzi. : "kwa kusudi la kumshukuru Yahweh"

lazima nyama italiwa...kinaweza kuliwa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ni lazima aile hiyo nyama...anaweza kuila"

Leviticus 7:17

katika siku ya tatu

ya tatu hii ni namba ya kawaida kwa tatu. : "baada ya siku mbili"

lazima ichomwe moto

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. " : "mtu anayepaswa uiteketeza"

Iwapo kipande chochote cha nyama hiyo ya dhabihu kinachobaki kinaliwa katika siku ya tatu

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "iwapo mtu yeyote anakula nyama yake ya sadaka

hakitakubalika

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Yahweh hataikubali"

wala hakitatolewa kwa aliyeitoa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "wala Yahweh hataiheshimu dhabihu ambayo huyo mtu aliitoa"

atabeba hatia ya dhambi mwenyewe yake

Mtu anayewajibika kwa dhambi aliyoitenda anazungumziwa kana kwamba anapaswa kubeba kimaumbile hiyo hatia.

Leviticus 7:19

9Nyama yoyote igusayo kitu kilicho najisi haitaliwa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Hakuna awezaye kula nyama inayogusa kitu fulani kilichonajisi"

kitu kilicho najisi

Kitu fulani ambacho Yahweh amekitamka kuwa hakifai kukigusa au kukila kinasungumziwa kana kwamba kilikuwa najisi kimaumbile.

Ni lazima iteketezwe kwa moto

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yapasa uiteketeze kwa moto"

yeyote aliye safi

Mtu mwenye kukubalika kwa kusudi la Mungu anazungumziwa kana kwamba ni mtu aliyekuwa safi kimaumbile.

mtu yeyote aliyenajisi

Mtu asiyekukubalika kwa kusudi la Mungu anazungumziwa kana kwamba ni mtu aliyekuwa mchafu kimaumbile.

yapasa mtu huyu akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake.

Mtu anayetengwa kutoka kwa jamii yake anazungumziwa kana kwamba amkwisha kukatwa kutoka kwa watu wake, kama vile mtu akatavyo kipande cha nguo au tawi kutoka kwenye mti. : "mtu huyo hawezi kuishi miongoni mwa watu wake" au "yapasa umtenge mtu huyo kutoka kwa watu wake"

Leviticus 7:21

kitu chochote kilichonajisi

Kitu fulani ambacho Yahweh amekitaja kuwa hakifai kugusa au kula kinazungumziwa kana kwamba kilikuwa si safi kimaumbile.

iwe ni unajisi wa binadamu, au wa mnyama aliyenajisi,

"Mtu" hapa mumaanisha wanadamu kwa ujumla. : "ikiwa wa mtu au wa mnyama

au wa kitu fulani kilichonajisi na chenye kuchukiza

au wa unajisi fulani wa kitu ambacho humchukiza Yahweh

lazima mtu huyo akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake.

Tazama maelezo katia sura ya 7:19. Hii pia yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji.

Leviticus 7:22

Kisha Yahweh akazungumza na Musa, akisema, "Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, 'hamruhusiwi kula mafuta

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Nukuu ya moja kwa moja yaweza kutamkwa kama nukuu taarifa yenyekutajwa. "Kisha Yahweh na akamwambia Musa kumbia kuwaambia watu wa Israeli kwamba: "Hamtakula mafuta"

afaye peke yake bila ya kuwa dhabihu

"aliyekufa peke yake lakini hakuwa dhabihu"

mafuta ya mnyama yeyote aliyeraruliwa na wanyama pori

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "mafuta ya mnyama yule ambaye mnyamapori alimuua"

Leviticus 7:25

dhabihu iliyofanywa...kwa moto

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Sadaka ya kutekeza"

mtu huyo lazima atakatiliwa mbali kutoka kwa watu wake

Tazama katika sura ya 7:19

Hamtakula damu

"Hamtatumia damu"

katika mojawapo ya nyumba zenu

"katika masikani yenu" au "popote mwishipo"

Leviticus 7:28

Kwa hiyo Yahweh akazungumza na Musa na akasema, "Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, 'Yeye atoaye

Hii ina nukuu ndani ya nukuu. Nukuu ya moja kwa moja yaweza kutamkwa kama nukuu taarifa yenyekutajwa. : Kisha Yahweh akazungumza na Musa na akamwambia awaambie watu wa Israeli kwamba: 'Yeye atoaye"

Mikono yake mwenyewe lazima iilete hiyo sadaka ifanywayo kwa Yahweh kwa moto

Kile kirai "ifanywayo kwa moto" yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Yeye mwenyewe analazimika kuileta sadaka anayopanga kuiteketeza kama dhabihu kwa Yahweh"

Mikono yake mwenyewe

"Mikono" humwakilisha mtu mzima. : "yeye mwenyewe anapaswa kuileta"

kidari

Sehemu ya mbele ya mwili wa mnyama iliyoko chini ya shingo

ili kwamba kidari kiweze kutikiswa kuwa sadaka ya kutikiswa mbele za Yahweh.

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ili kwamba kuhani aweze kuiwasilisha kwa Yahweh kama sadaka ya kutikiswa"

kiweze kutikiswa kuwa sadaka ya kutikiswa mbele za Yahweh.

Kuiinua juu sadaka ni mfano wa ishara unaoonyesha kwamba mtu anaiweka wakfu dhabihu kwa Yahweh.

Leviticus 7:31

Paja

Sehemu ya juu ya mguu juu ya goti

kama sadaka iliyotokana

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "nawe uitoe kama sadaka"

Leviticus 7:33

Kwa kuwa nimetwaa

"Nime..." hapa humrejelea Yahweh.

uwe mchango

hiyo ninaitoa kama sadaka"

Leviticus 7:35

sadaka zilizofanywa kwa Yahweh kwa moto

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Sandaka za kuteketezwa kwa ajili ya Yahweh"

ambao Yahweh aliamru waweze kupewa kutoka kwa watu wa Israel

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "aliyowaamru Yahweh watu wa Israeli kuitoa kwao"

hiyo aliyowatia mafuta ya upako wawe makuhani

ambayo Musa aliwapaka mafuta makuhani".

katika vizazi vyote

Hii yaweza kufasiriwa kama katia sura ya 3:15

Leviticus 7:37

Maelezo Unganishi

Huu ni mwisho wa hotuba iliyoanzia katika 7:28

Leviticus 8

Leviticus 8:1

Taarifa kwa ujumla

Katia sura ya 8 Musa anawaweka wakfu Aroni na wanawe wawe makuhani kulingana na aagizo ya Yahweh ambayo aliyaamru katika kitabu cha Kutoka

mavazi

"Mavazi ya kikuhani" au "nguo walizavaa makuhani"

Leviticus 8:4

Haya ndiyo Yahweh amegiza yatendwe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Yahweh alituamru sisi kutenda"

Leviticus 8:6

na kuwaosha kwa maji

Hili ni tendo la kiishara. Ni usafishaji wa kiibada ambao huwandaa wao kuwa makuhani.

kanzu... ukumbuu...joho...kizibao...mshipi uliosokotwa kwa ustadi

mshipi uliosokotwa kwa ustadi - Haya ni mavazi ambayo Yahweh aliwaamru watu kutengeneza kwa ajili ya makuhani.

ukumbuu`

kipande cha nguo kirefu ambacho kinafungwa kuzunguka kiuno au kifua.

kukikaza mwilini mwake

"alikifunga kumzunguka"

Leviticus 8:8

akaweka kifuko kifuani mwa Aroni

"Musa aliweka kifuko juu ys |Aroni"

kifuko kifuani..kiremba...bamba la dhahabu... taji takatifu

Haya yote ni mavazi maalum ambayo Yahweh aliwaamru watu kutengeneza kwa ajili ya makuhani.

Urimu na Thumimu

Hivi havikujulikana wazi vilikuwa ni vitu gani. Vilikuwa vitu ambavyo kwa kuhani alivitumia kwa namna fulani kupambanua mapenzi ya Mungu.

kiremba

kifuniko cha kicho cha mtu ambapo kilikuwa ni kitambaa cha nguo kirefu kilichofungwa kukizunguka kichwa

bamba la dhahabu; liwe taji takatifu

Virai hivi viwili hurejelea kitu kile kilekile. Lilikuwa ni mamba la dhahabu tupu lililoambatanishwa na kiremba.

Leviticus 8:10

vyombo vyake vyote

Hivi vyote ni vyungu, masufuria, makoleo, na nyuma vilivyotukaka kwenye madhabahu.

sinia la kunawia

Hili ni besenni la shaba liliowekwa kati ya madhabahu na hema.

kitako chake

Hiki ni kinara cha shaba ambacho juu yake sinia la kunawia liliwekwa.

Leviticus 8:12

Akamimina

"Musa alimimina"

ukumbuu

Tazama lilivyofasiriwa katika sura ya 8:6

Leviticus 8:14

wakaweka mikono yao juu ya kichwa

Tazama jinsi lilivyofasiriwa katika sura ya 1:3

mpembe za madhabahu

Tazama jinsi lilivyofasiriwa katika sura ya 4:6

kuitenga kwa Mungu

"tenga madhabahu kwa ajili ya Mungu"

kufaa kwa kufanyia upatanisho.

"Upatanisho" hapa humaanisha kuifanya madhabahu ifae katika kumtumikia Mungu. : "ili kuifanya mahali pa kufaa kwa ajili ya kuteketezea dhabihui ya dhambi"

Leviticus 8:16

sehemu za ndani

Tazama lilivyofasiriwa katika sura ya 1:7

ini...figo

Tazama lilivyofasiriwa katika sura ya 3:3

ngozi

Hili ni vazi au nyama ya juu yenye manyoya ya mwili wa mnyama wa kundini

Leviticus 8:18

wakaweka mikono yao juu ya kichwa

Tazama lilivyofasiriwa katika sura ya 1:3

Leviticus 8:20

Naye akamkatakata kondoo

"Musa akamkata kondoo"

ilitoa harufu ya kupendeza

Tazama lilivyofasiriwa katika sura ya 1:7

sadaka iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Sadaka aliyoiteketeza kwa Yahweh"

Leviticus 8:22

kondoo wa kuwekwa wakfu

Neno "kuweka wakfu" ni nomino dhahania. : "kondoo kwa ajili ya kuwatenga Aroni na wanawe kwa ajili ya huduma ya Mungu"

wakaweka mikono yao juu ya kichwa

Tazama lilivyofasiriwa katika sura ya 1:3

naye akaweka sehemu ya damu ya kondoo

Inaonesha kwamba Musa aliikinga damu kwenye bakuli wakati ilipochuruzika kutoka kwa mnyama. Maana yake yaweza kuwekwa wazi

Leviticus 8:25

sehemu za ndani

Tazama lilivyofasiriwa katika sura ya 1:7

ini...figo

Limefasiriwa kama ilivyofanyika katika sura ya 3:3

paja la kulia

Tazama lilivyofasiriwa katika sura ya 7:31.

kikapu cha mikate isiyo na hamira ambayoo ilikuwa mbele za Yahweh

Hii haimaanishi mahali pa kikapu cha mikate. humaanisha kwamba huu ni mkate ambao Musa amishauweka wakfu kwa Yahweh.

weka mikoni mwa Aroni na katika mikono ya wanawe

"Mikono" hapa huwakilisha nafsi nzima. : "aliitoa yote kwa Aroni na wanawe"

kuvitikisa mbele za Yahweh kuwa sadaka ya kutikiswa

Inaashiria kwamba Aroni na wanawe waliiwasilisha sadaka. Maana kamili ya tamko hili yaweza kufanywa ya kueleweka. :"Walivitikisa mbele za Yahweh kuwa sadaka ya kutikiswa"

kuitikisa

Hili ni tendo la kiishara linaloweka wakfu sadaka kwa Yahweh.

Leviticus 8:28

Musa akaichukua

sherehe rasmi inayomfanya mtu kuwa kuhani

kutoka mikononi mwao

"Mikono" hapa huwakilisha nafsi nzima. : "kutoka kwa Aroni na wanawe"

Zilikuwa ni sadaka ya kuwekwa wakfu

"Zilikuwa sadaka za kuwatenga Aroni na wanawe kwa ajili ya huduma kwa Yahweh"

sadaka iliyofanywa kwa Yahweh kwa moto

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Sadaka ya kuteketezwa kwa Yahweh kwa moto

ilitoa harufu ya kupendeza

Tazama lilivyofasiriwa katika sura ya 1:7

kidari

Sehemu ya mbele ya mwili wa mnyama chini ya shingo

kuwekewa mikono

Sherehe rasmi inayomfanya mtu kuwa kuhani

Leviticus 8:30

Musa

Musa alikuwa nabii na kiongozi wa watu wa Musa alipokuwa mtoto, wasazi wake Musa walimweka kwennye kikapu kwenye mianzi ya mto Nile ili kumficha kutoka kwa Pharao wa Misri. Miriamu, dada yake Musa alimwangalia huko. Maisha ya Musa yalilindwa tu pale binti Farao alipomwona na kumpeleka ikulu kumlea kama mwanawe.

Mungu allimchagua Musa kuwaokoa Waisraeli kutoka utumwani Misri na kuwaongoza mpaka nchi ya ahadi.

Baada kuundoka kwa Waisraeli huko Misri, na wakiwa wanarunguka jangwani, Mungu alimpa Musa mbao mbili za mawe zilizoandikwa Amri za Mungu juu yake.

Karibu na mwisho wa uhai wake, Musa aliitazama tu nchi ya ahadi, lakini hakuingia kuishi humo kwa sababu hakumtii Mungu.

Paka mafuta, mpakwa mafuta

Neno "paka mafuta" humaanisha kusugua au mimina mafuta juu ya mtu au chombo, Wakati mwingine mafuta yalichanganywa na viungo, vikiyapa harufu yenye manukato. Neno pia limetumika kitamathari kumaanisha Roho Mtakatifu kumchaguwa na kumwezesha tu.

Katika Agano la Kale, makuhani, wafalme na manabii walipakwa mafuta ili kutenga kwa huduma maalum kwa Mungu.

Vyombo kama vile madhababhuau hema, vilipakwa mafuta kuonyesha kwamba vilikuwa vitumike kumwabudia na kumtukuza Mungu.

Katika Agano Jipya, wagonjwa walipakwa mafuta kwa uponyaji wao.

Agano Jipya hutaarifu mara mbili amabapo Yesu alipopakwa yenye manukato na wanawake, kama tendo la ibada. Wakati mmoja Yesu alisifia kwamba kwa kufanya hivi mwanamke huyo alikuwa akiandaa maziko Yake ya baadaye.

Yesu alipokufa, rafiki zake waliuandaa mwili wake kwa maziko kwa kuupaka mafuta na uvumba.

Vyeo "Mesiya" (Kiebrania) na "Kristo" (Kiyunani) humaanisha "Mpakwa mafuta"

MAPENDEKEZO YA UFASIRI

Kutegemeana na muktadha, neno "paka mafuta" laweza kufasiriwa kama "mimina mafuta juu ya" au "weka mafuta juu ya" au "weka wakfu kwa kumminia mafuta yaliyotiwa manukato."

"Kupakwa mafuta" laweza kufasiriwa kama "wekwa wakfu kwa kupakwa mafuta." au "teuliwa" au "wekwa wakfu."

Katika baadhi ya mazingira neno "paka mafutaa" linaweza kufasiriwa kama "teuwa."

Kirai kama "kuhani mpakwa mafuta," laweza kufasiriwa kama "kuhani aliyewekwa wakfu kwa mafuta" au kuhani aliyetengwa kwa miminiwa mafuta juu yake."

damu

Neno "damu" humaanisha kimiminika chekundu ambacho hutoka katika ngozi ya mtu kunapoukuwa na jeraha au kovu. Damu hutoa virutubisho viletavyo uhai katika mwili mzima wa mtu.

Damu huashiria uhai na inapomwagwa, huashiria kupoteza maisha au kifo.

Watu walipofanya dhabihu kwa Mungu, waliua mnyama na walimimina damu juu ya madhabahu. Hii iliifananisha dhabihu ya uhai wa damu ya mnyama

Mafuta

Mafuta ni kimiminika kizito, safi kilichotokana na mimea au matunda fulani. Kwa kawaida katika nyakati za Biblia yalitokana na mizeituni.

Mafuta ya zeituni yalitumika kwa kupikia, kupaka, dhabihu, taa, na dawa.

katika nyakati za kale, mafuta ya zeituni yalikuwa na gharama kubwa na umiliki wa mafuta ulihesabika kama kipimo cha utajiri.

Madhabahu

Madhabahu ni muundo ulionuliwa juu ambao juu yake Waisrali waliteketeza wanyama na nafaka kama sadaka kwa Mungu.

Nyakati za Biblia, mara kwa mara watu walitengeneza madhabahu rahisi kwa kuumba rundo la undongo uliofungashwa au kwa kupanga mawe makubwa kwa ungalifu ili kufanya rundo imara.

Baadhi ya madhabahu zilitengenezwa kwa kuunda makasha maalum kwa mbao zilizofunikwa kwa metali kama vile dhahabu, shaba nyeupe au shaba nyekundu.

Baadhi ya makundi mengine ya watu jirani na Israeli pia walijenga madhabahu ili kutoa dhabihu kwa miungu yao.

tenga

Neno "tenga" humaanisha kutengwa na jambo fulani ili kutimiza kusudi fulani.

Waisraeli walitengwa kwa huduma ya Mungu.

Roho Mtakatifu aliwaamru Wakristo wa Antiokia kuwatenga Paulo na Barnaba kwa kazi ya Mungu aliyowataka wao waifanye.

Mwamini "aliyetengwa" kwa kazi ya Mungu "amewekwa wakfu" kutimiza mapenzi ya Mungu.

Moja ya maana ya "mtakatifu" ni kutekwa kuwa wa Mungu na kuwa umetengwa kutoka katika njia za dhambi za ulimwengu.

Ule msamiati "takasa" humaanisha kumtenga mtu kwa huduma ya Mungu.

MAPENDEKEZO YA UFASIRI Njia za kufasiri "kutenga" zaweza kujumuisha, "kuchagua mahususi" au kutenga kutoka miongoni mwenu" au "kuweka kando ili kufanya kazi maalum."

"Kutengwa" kwaweza kufasiriwa "kuwekwa kando

Vaa, vikwa

Neno "kuvikwa na" linapotumika kitamathli kwenye Biblia, humaanisha kuruzukiwa au kuandaliwa kwa kitu fulani. "Kujivika" mwanyewe na kitu fulani humaanisha kutafuta kuwa na tabia yenye sifa fulani.

MAPENDEKEZO YA UFASIRI Kama inawezekana, ni vema kuitunza tamathali ya usemi, "jivike na." Njia nyingine ya kufasiri hili ni yaweza kuwa "vaa" kama hii ingemaanisha kuvaa nguo.

Kama hii haileti maana sahihi, njia nyingine ya kuifasiri tamathali "kuvikwa na" yaweza kuwa "kuonyesha" au "kudhihirisha" au kujazwa na" au kuwa na sifa ya."

Neno "jivike na" laweza pia kufsiriwa kama "jifunike na" au "enenda katika njia ambayo huonyesha."

mwana, mwana wa

Neno "mwana" hurejelea mvulana au katika uhusiano kwa wazazi. Laweza pia kumaanisha ama mzao mwanaume wa mtu fulani au kwa mwana aliyeasiliwa.

"Mwana," mara kwa mara limetumika kimafumbo katika Biblia kumaanisha mzao yeyote wa kiume, kama vile mjukuu au kitukuu.

Neno "mwana" pia linaweza kutumika kama muundo wa kistaraabu wa kumwita mvalana au mtu aliye kijana.

Wakati mwingine "wana wa Mungu" limetumika kwenye kumaanisha waaminio katika Kristo.

Mungu anaiita Israeli "mwanawe mzaliwa wa kwanza." Hii hurejelea uchaguzia wa Mungu wa taifa la Israeli kuwa watu maalum wa Mungu. Ni kwa kupitia kwao kwamba ujumbe wa ukombozi na wokovu ulikuja, ukiwa na matokeo yake kwamba watu wengi wamefanyika watoto wa kiroho.

Kirai "mwana wa" mara kwa mara limekuwa na maana ya kimafumbo, "kikiwa na sifa bainishi za." Mifono ya hiki hujumuisha wana wa nuru," "wana wa amani," na "wana wa ngurumo."

Kirai "mwana wa" pia kimetumika kuzungumzia ni nani aliye baba wa mtu. Kirai hiki hutumika kuelezea vizazi na maeneo mengine mengi.

Kwa kutumia "mwana wa" kwa kutoa jina la baba mara mara husaidia kutofautisha watu wenye majina yenye kufanana. Kwa mfano, "Azaria, mwana wa Sadoki" na Azaria, mwana wa katika 1 Wafalme 4, na "Azaria, mwana wa Amazia" katika 2 Wafalme 15 ni watu watatu waliotofauti.

MAPENDEKEZO YA UFASIRI Kwenye muktadha wa kukiri kwamba kitu fulani ni kweli, "kiri" laweza kufasiriwa kama "kubali" au "tangaza" au "ungama" kuwa ni kweli au "amini."

Linapomaanisha kumtambua mtu, neneo hili laweza kufasiriwa kama "pokea" au "tambua" uthamni wa" au ambia wengine kwamba

Leviticus 8:31

kikapu cha kuwekwa wakfu

Hii humaanisha kikapu kilicho na matoleo yatumikayo wakati wa kuwaweka wakfu Aroni na wanawe. : "kile kikapu"

kama nilivyoamru, kusema, 'Aroni na wanawe wataila

Hii ina nukuu ndani ya nukuu. Nukuu ya moja kwa moja yaweza kutamkwa kama nukuu isiyo ya moja kwa moja. " kama nilivyokuagiza kufanya"

hata zitakapotimia siku za kuwekwa mikono kwenu

Hii yaweza kufasiriwa katiika mtindo wa utendaji. : "mpaka mkamilishe siku zenu za kuwekewa mikono.

kuwekwa mikono

Tazama lilivyofasiriwa katika sura ya 8:28

Leviticus 8:34

Kitendeke

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "sisi tutende"

Kufanya upatanisho kwa ajili yenu

Ile Nomino dhahania "upatanisho" yaweza kutamkwa kama kitenzi. : " Kupatanisha kwa ajili ya dhaambi zenu"

hivi ndivyo nimeamriwa

Hii yaweza kufasiriwakatika mtindo wa utendaji. "hivi ndivyo ameniamru"

Leviticus 9

Leviticus 9:1

siku ya nane

Neno "ya nane" ni namba ya kawaida kwa nane.

Mbele za Yahweh

"kwa Yahweh" au "katika uwepo wa Yahweh"

Leviticus 9:3

Maelzo jumla:

Musa anaendelea kumwambia Aroni'

Zungumza na watu wa Israeli na uwaambie, 'Twaeni beberu...atajidhihirisha kwenu

Musa anaendelea kumwambia Aroni. Sentensi hii ina nukuu ndani ya nukuu. Nukuu ya moja kwa moja kwa moja yaweza kutamkwa kama nukuu taarifa iliyotwa. : "na waambie watu Israeli watwae beberu...atajidhihirisha kwa watu wote"

wa umri wa mwaka moja

"mwenye umri wa miezi kumi na miwili"

ilikuwatoa mbele za Yahweh

"kutoa kwa Yahweh"

Leviticus 9:6

amewaamru nyinyi mfanye

"Nyinyi" hapa humaanisha watu wa Israeli.

ili kwamba utukufu wake uweze kuonekana kwenu

"Utukufu" hapa huwakilisha uwepo wa Yahweh. : ""ili kwamba aweze kuonyesha utukufu wa uwepo wake"

kufanya upatanisho kwa ajili yako mwenyewe.. na kwa ajili ya watu ili kufanya upatanisho kwa ajili yao

Hizi ni dhabihu mbili tofauti. Dhabihu ya kwanza ni kupatanisha kwa ajili ya dhambi za kuhani mkuu. Kuhani mkuu anapotenda dhambi, hiyo dhambi huwafanya watu wawe na hatia. (Tazama 4:1) Dhabihu ya pili ni kupatanisha dhambi za watu wanazotenda wenyewe.

Leviticus 9:8

wana wa Aroni wakamletea hiyo damu

Hii inaonyesha kwamba waliikinga damu kwenye bakuli wakati damu ilipokuwa ikichuruzika kutoka kwa mnyama. Maana kamili ya tamko hili yaweza kufanywa wazi wazi

pembe za madhabahu

Tamza maelezo ya sura ya 4:6

chini ya kitako cha madhabahu

"chini ya madhabahu"

Leviticus 9:10

aliyateketeza

"Aroni aliiteketeza"

figo...ini

Tazama maelezo ya sura ya 3:3

ngozi

Tazama maelezo ya sura ya 7:7

Leviticus 9:12

wanawe wakampa hiyo damu

Tazama maelezo ya sura ya 9:8

sehamu za ndani

Tazama maelezo ya sura ya 1:7

Leviticus 9:15

mbuzi wa kwanza

Neno "wa kwanza" ni namba ya mpango kwa ajili ya namba moja. : "mbuzi kwa ajili ya sadaka yake mwenyewe.

pamoja na sadaka ya asubuhi ya kuteketezwa

Hii humaanisha dhabihu ya kwanza ya kila siku. kuhani angieitoa dhabihu hii ya kuteketezwa asuhubi kabla ya dhabihu nyingine yot yote. Maana kamili yaweza kufanywa wazi.

Leviticus 9:18

Akamchinja

"Aroni alichinja"

wana wa Aronni wakampa damu

Inamaanisha kwamba damu ilikuwa kwenye bakuli. Maana kamili yaweza kufanywa wazi.

Sehemu za ndani

Tazama maelezo ya sura ya 1:7

figo...ini

Tazama maelezo ya sura ya 3:3

Leviticus 9:20

Wakazichukua hizi sehemu

"wana wa Aroni walizichukua hizo sehemu"

wakaziweka hizi

Neno "hizi" hurejelea mafuta na sehemu zilizoorodheshwa hapo awali.

vidari

Tazama amaelezo ya sura ya 7:28

paja la kulia

Tazama amaelezo ya suru ya 7:31

mbele za Yahweh

"kwa Yahweh"

Leviticus 9:22

kisha akashuka chini

Kirai "akashuka chini" kimetumika kwa sababu mahali pa madhabahu palikuwa juu zaidi ya mahali watu walipokuwa wanasimama.

utukufu wa Yahweh ukaonekana kwa watu wote

"Utukufu" hapa huwakilisha uwepo wa Yahweh. : "Yahweh akawaonyesha watu wote utukufu wa uwepo wake"

Moto ukashuka kutoka kwa Yahweh na ukairamba

"Yahweh alituma moto ulioiramba"

ukairamba sadaka ya kuteketezwa

Moto ukiitekeza kabisa sadaka umezungumziwa kana kwamba moto uiitafuna au kuitumia sadaka ya kutekezwa.

wakala wakiinamisha nyuso zao chini

"walilala wakaelekeza nyuso zao ardhini." Hii ni ishara ya heshima na adhama.

Leviticus 10

Leviticus 10:1

Nadabu na Abihu

Haya ni majina ya wana wa Aroni

kifukizo

chombo cha metali chenye kina kifupi ambacho makuhani walikitumia kubebea makaa ya moto au uvumba

wakakaweka moto ndani yake

"akaweka makaa yaliyowaka moto ndani yake"

wakatoa moto usiokuabalika mbele za Yahweh, moto ambao hakuwaamru wao kuutoa

"Lakini Yahweh hakuikubali sadaka yao kwa sababu haikuendana na kile ambacho aliwaamru kukitoa"

moto usiokuabalika mbele za Yahweh

"moto usiokubalika kwa Yahweh"

Kwa hiyo moto ukashuka chini mbele za Yahweh

"Kwa hiyo Yahweh akatuma moto"

ukashuka chini mbele za Yahweh

"ulikuja kutoka kwa Yahweh"

na kuwala

Moto ukiwaunguza kabisa watu unazungumziwa kana kwamba uliwala au uliwatumia kabisa.

nao wakafa mbele za Yahweh

"walikufa katika uwepo wa Yahweh"

Leviticus 10:3

"Hiki ndicho Yahweh alichokuwa akikiongelea aliposema, 'Nitaufunua utakatifu wangu... mbele za watu wote'"

Hii ina nukuu ndani ya nukuu. Nukuu halisi yaweza kutamkwa kama nukuu taarifa iliyotajwa. : "Hiki ndicho Yahweh alichokuwa akiongelea alliposema kwamba angefunua takatifu wake...wamkaribiao yeye, na ya kwamba yeye atatukuzwa...watu

Nitaufunua utakatifu wangu kwa wale wanikaribiao

Kile kirai "wale wanikaribiao" humaanisha makuhani wamtumikiao Yahweh. "Nitawaonyesha wale ambao hukaribia kunitumikia kwamba Mimi ni mtakatifu" au "Wale wanaokuja karibu ili kunitumikia lazima wanitendee kama mtakatifu.

Nami nitatukuzwa mbele za watu wote

Sehemu hii ya pili ya tamko la Yahweh bado linamhusu kuhani, ambaye ni mmoja wa wanaomkaribia Yahweh. "Laazima wanitukuze mbele za watu wote" au "Lazima waniheshimu katika uwepo wa watu wote"

Mishaeli...Elzafani...Uzieli

Haya ni majina ya watu

ndugu zenu

Hii haimanishi kwamba walikuwa ndugu halisi. "Ndugu" hapa humaanisha jamaa au binamu.

Leviticus 10:5

Hivyo wakakaribia

"Kwa hiyo Mishaeli na Elzafani wakakaribia"

kuwachukua wangali wamevaa kanzu zao za kikuhani

Waliibeba miili ya Nadabu na Abihu, ambayo ilikuwa ingali kwenye kanzu za kikuhani

Eliezari...Ithamari

Haya ni majina ya wana wa Aroni.

Msiache wazi nywele za vichwa vyenu, wala msirarue nguo zenu,

Yahweh anawaambia Aroni na wanawe wasionyeshe ishara yoyote ya nje ya huzuni au kuomboleza.

ili kwamba msije mkafa

"ili kwamba msife"

asilikasirikie kusanyiko zima

"Kusanyiko" hapa humaanisha kutaniko zima la Israeli, siyo kikundi cha viongozi tu. : "asiwakasirikie watu wote wa Israeli"

nyumba yote ya Israeli

"Nyumba" hapa huwakilisha watu wa Israeli. "watu wote wa Israeli"

kwa ajili ya hao ambao Yahweh amewaangamiza kwa moto

"kwa ajili ya wale ambao Yahweh aliwaua kwa moto wake"

Leviticus 10:8

Hii itakuwa

"Hii" hapa hurejea nyuma kwenye amri kwa ajili ya makuhani ya kutokunywa mvinyo na kinywaji kikali waingiapo kwenye hema la kukutania.

amri ya kudumu katika vizazi vyote vya watu wenu

Tazama maelezo ya sura ya 3:15.

ili kupaambanua

Unaweza kuanza sentensi mpya hapa. "Yawapasa mfanye hivyo ili kwamba muweze kutofautisha"

kati ya mambo matakatifu na mambo ya kawaida

Yale majina vumishi "mataktifu" na "ya kawaida" yaweza kutamkwa kama vivumishi. : "Kati ya kilicho kitakatifu na "cha kawaida" au "kati ya kilichowekwa wakufu kwa Mungu na kilicho cha kawaida

kati ya kilichonajisi na kilichosafi

Yale majina vumishi "kilichonajisi|" na "kisichosafi" yaweza kutamkwa kama vivumishi. : "Kati ya kinajisi na kisafi" au "kati ya kile Mungu ambacho Mungu hatakikubali na kile ambacho atakikubali"

Kilichonajisi

Mtu au kitu ambacho Yahweh amekitamka kuwa hakifai kuguswa yanazungumziwa kana kwamba yalikuwa kichafu kimaumbile.

kilichosafi

Mtu au kitu ambacho Yahweh amekitamka kuwa hakifai kuguswa yanazungumziwa kana kwamba yalikuwa safi kimaumbile.

Leviticus 10:12

sadaka ifanywayo kwa Yahweh kwa moto

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Sadaka za kuteketezwa kwa Yahweh"

kwa kuwa ni takatifu sana

"kwa kuwa sadaka ya nafaka ni takatifu sana"

hivi ndivyo nimeamriwa kuwaambia ninyi

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa tendakji. : "hivi ndivyo Yahweh ameniamru kuwaambia ninyi"

Leviticus 10:14

Kile kidari kitikiswacho na lile paja ambalo hutolewa kwa Yahweh

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "kile kidali na paja ambalo mtu alilitikisa na kuipeleka kwa Yahweh"

kidari

ile sehemu ya mbele ya mwili wa mnyama chini ya shingo

paja

ile sehemu ya juu mguu juu ya goti

Wewe mwenyewe, wanao na binti zako

"Wewe" hapa humaanisha Aroni

Nazo zitakuwa zako wewe na wanao uwe mgao wenu daima

Hii ijulikane kwamba sehemu hiyo ni ya Aroni na wanawe. : "Sehemu hii daima itakuwa kwa ajili yako na wanao"

Leviticus 10:16

ametekezwa kwa moto

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Kuhani alikuwa ameiteketeza yote"

Eleazari and Ithamari

Yafasiri majina haya kama yalivyofasiriwa katika sura ya 10:5

Kwa nini hamjaila ... mbele zake?

Musa anatumia swali kuwakemea Eleazari na Ithamari. swahili hili lenye ufsaha laweza kufasiriwa tamko. : "Iliwapasa kuwa mmeila...mbele zake."

kwa kuwa ni takatifu sana

"kwa kuwa sadaka ya dhambi ni takatifu sana"

kuchukua uovu wa kusanyiko

Ikimsababisha Yahweh kuwasamehe watu wa Israeli kunazungumziwa kana kwamba uovu ulikuwa kitu ambacho Yahweh hukichukua kutoka kwa watu.

mbele zake

"katika uwepo wake"

Tazama, damu yake haikuletwa ndani ya hema

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "hukuileta damu yake"

Leviticus 10:19

jambo hili vilevile limetendeka kwangu

Aroni anarejea kwa kifo cha wanawe wawili.

Isingekuwa imeshapendeza mbele za Yahweh?

Dhabihu hizi zilikuwa za kuliwa kwa shangwe na furaha. Aroni anatumia swali kusisitiza kwamba Yahweh asingekuwa amependezwa naye kwa kula dhabihu kwa kuwa anahuzuni kwa sababu ya vifo vya wanawe. Swali hili laweza kufasiriwa kama tamko. : "hakika Yahweh asingekuwa amependezwa."

Leviticus 11

Leviticus 11:1

miongoni mwa wanyama

"kutoka kwa wanyama wote"

Leviticus 11:3

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile anawachoruhusu watu kula na kile ambacho anawazuia kula.

kwato zenye kugawanyika

Hii humaanisha kwamba kwato zilizogawanyika sehemu mbili badala ya kuwa wayo mmoja

hucheua.

Hii humaanisha mnyama anayeleta chakula kinywani kutoka tumboni mwake na hukitafuna tena.

aadhi ya wanyama ambao ama hawacheui au hana kwato zilizogawanyika

Yaani kwamba, wana moja au nyingine, lakini siyo yote mawili.

ngamia ni najisi kwenu

Ngamia kuwa hafai kwa watu kumla amaezungumziwa kana kwmaba alikuwa mchafu kimaumbile.

Leviticus 11:5

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwambia Musa na Aruni kile anachowaruhusu watu kula na kile ambacho anawakataza kula.

Pimbi

Mnyama mdogo aishiye maeneo ya miamba.

najisi kwenu

wanyama hawa ambao Mungu amewatamka hawafai kwa watu kuwala wamezungumziwa kana kwamba walikuwa wachafu kimaumbile.

Sungura

Mnyama mdogo mwenye manyoya marefu ambaye kwa kwaida huishi kwenye mashimo chini ardhini.

wala msiiguse mizoga yao

"wala msiguse miili yao iliyokufa"

Leviticus 11:9

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwambia Musa na Aruni kile anachowaruhusu watu kula na kile ambacho anawakataza kula

Mapezi

pezi , ni sehemu iliyobapa ambayo samaki huitumia kuogelea majini.

Magamba

Ni mabamba madogo madogo yanayoufunika mwili wa samaki.

viumbe wote hai wasio na mapezi na magamba waliomo baharini au mitoni

"wanyama wote waishio baharini au mitoni wasio na mapezi na magamba"

watakuwa chukizo kwenu

Yahweh anawaamru watu kuwakataa na kudharau kuwal a viumbe hawa. Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yapsa mwawachukie hao" au "lazima mukatae kabisakabisa"

Leviticus 11:11

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwambia Musa na Aruni kile anachowaruhusu watu kula na kile ambacho anawakataza kula

Kwa kuwa watakuwa chukizo

"kuchukia" ni kukitaa na kukidharamu kitu. Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo" wa utendaji. : "kwa kuwa yawapasa kuwachukia hao au kwa kuwa ni lazima muwakatae kabisakabisa"

mizoga yao sharti itakuwa chukizo

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ywapasa kuichukia miili yao iliyokufa" au "msiguse miili yao iliyokufa"

Chochote kisichokuwa na mapezi au magamba kilichomo majin

"Chocote kilichomo majini kisichokuwa na mapezi na magamba"

lazima kiwe chukizo kwenu

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "lazima mvichukie" au "lazima mvikatae kabisa kabisa"

Leviticus 11:13

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwambia Musa na Aruni kile anachowaruhusu watu kula na kile ambacho anawakataza kula

tai, furukombe, kipungu, mwewe mwekundu, aina yoyote ya kipanga, kila aina ya kunguru, 16kiruka-njia, kipasuasanda, Shakwe..aina yoyote ya mwewe.

Kuna ndege ambao ama hukaa macho usiku au hula panya na wanyama waliokufa.

Leviticus 11:17

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwambia Musa na Aruni kile anachowaruhusu watu kula na kile ambacho anawakataza kula

bundi mdogo...bundi mkubwa...chukizo, mnandi, bundi mweupe na mwari, korongo...ina zote za koikoi, huduhudi...popo

Hawa ndege walao panya na wadudu na aghalabu hukaa macho usiku

bundi mkuu

""bundi mkubwa"

Koikoi...huduhudi

Hawa ni ndege walao panya na mijusi.

popo

Ingawaje popo si ndege, kwenye orodh hii popo ni najisi kwa sababu ana mabawa na huruka. ana mwili wa manyoya na hasa hukaa macho usiku. Yeye hula wadudu na panya

Leviticus 11:20

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwambia Musa na Aruni kile anachowaruhusu watu kula na kile ambacho anawakataza kula

Wadudu wote wenye mabawa wanaotembea kwa miguu minne ni machukizo kwenu

Neno hili "chukuzo" laweza kufasiriwa na kirai che kitenzi. : "Mtawachukia wadudu wote wenye mabawa wanaotembeao kwa miguu yao miine"

Wadudu watembeao kwa miguu minne

Kirai "miguu miine" hapa ni nahau inayomaanisha kutambaa juu ya ardhi na huwatenga wadudu hawa na vitu vingine virukavyo, kama vile ndege, ambao wana miguu miwili tu. : "wadudu wataambao juu ya ardhi"

nzige, senene, parare, au panzi.

Hawa ni wadudu wadogo ambao hula mimea na wanaweza kurukaruka.

wadudu warukao wenye miguu minne

"wadudu warukao walio na miguu miine"

Leviticus 11:24

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaanza kuwaambia Musa na Aroni ni wanyama gani ambao watu wanatakiwa kuwaona najisi.

Nanyi mtakuwa najisi hata jioni kutokana na wanyama hawa endapo mtagusa mizogo yao

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Miili ya wanya wanyama hawa waliokufa itawafanya nyinyi kuwa najisi kama mtagusa mmojawapo.

mtakuwa najisi

Mtu asiyekubalika kwa kusudi la Mungu kwa sababu amegusa mojawapo ya miili ya wanyama waliokufa anazungumziwa kana kwamba amekuwa si mchafu kimaumbile.

wanyama hawa

Hii hurejelea wanyama anaotaka kuwaorodheshaa katika mistari inayofuata.

Leviticus 11:26

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwambia Musa na Aruni kile anachowaruhusu watu kula na kile ambacho anawakataza kula

Kila myama...ni najisi kwenu

Hawa wanyama ambao Mungu amewataja kutofaa kwa kuliwa na watu wamezungumziwa kana kwamba walikuwa wachafu kimaumbile.

kwato zilizogawanyika

Tazama amelezo ya sura ya 11:3.

Cheuwa

Tazama maelezo ya sura ya 11:3

Kiala awagusaye atakuwa najisi

Mtu ambaye hakubaliki kwa makusudi ya Mungu kwa sababu ya amegusa mmojawapo wa wanyama hawa anazungumziwa kana kwamba alikuwa mchafu kimaumbile.

vitanga

Miuguu ya mnyama yenye makucha

hata jioni

"hata macheo"

Leviticus 11:29

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwambia Musa na Aruni wanyama ambao watu walitakiwa kuwaona najisi

hawa ndiyo walio najisi kwen

Hawa wanyama ambao Mungu amewataja kuwa hawafai kuguswa au kuliwa na watu wamezungumziwa kana kwamba walikuwa wachafu kimaumbile

kicheche

mnyama mdogo mwenye manyoya ya kahawia anayekula ndege na wanyama wadogo.

mijusi mikubwa, guruguru, 30kenge, mijusi ya ukutani...na kinyonga

Hizi ni aina mbali mabali za wanyama wenye damu baridi walio na miguu minne.

goromoe

"Mjusi wa ni"

Leviticus 11:31

Taarifa kwa Ujmla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aruni wanyama ambao watu walitakiwa kuwaona najisi

hawa ndiyo watakuwa najisi kw

Hawa wanyama ambao Mungu amewataja kuwa hawafai kuguswa au kuliwa na watu wamezungumziwa kana kwamba walikuwa wachafu kimaumbile

Yeyeote awagusaye...atakuwa najisi

Mtu ambaye hakubaliki kwa makusudi ya Mungu kwa sababu amegusa mmojawapo wa wanyama hawa anazungumziwa kana kwamba alikuwa mchafu kimaumbile

hata jioni

"hata macheo"

chombo hicho kitakuwa najisi

Chombo amacho Mungu amekitaja kuwa hakifai kwa watu kukigusa kwa sababu mwili wa mmojawapo wa myama hawa aliyekufa umeangua juu yake kimezungumziwa kana kwamba klikuwa kichafu kimaumbile. Kimezungumziwa kufaa baada ya kuwa kimeoshwa.

Kisha kitakuwa safi.

Kitu flani ambacho Mungu amekitaja kuwa kinafaa kwa watu kukiguza baada ya kuwa kimeoshwa kimeangumziwa kana kwamba kilikuwa safi kimaumbile.

lazima kitalowekwa katika maji

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "na vyovyote utakavyokitumia, itakupasa kukiloweka kwenye maji.

Leviticus 11:34

Vyakula vyote ambavyo ni safi

Vyakula ambavyo Mungu amevitaja kuwa vimekubalika kwa watu kula kimezumgumziwa kana kwamba kilikuwa safi kimaumbile.

na kilichoruhusiwa kuliwa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ambacho waweza kukila"

.nacho kitakuwa najisi

Chakula kisichokubalika kwa watu kukila kwa sababu maji yaliyonajisi yamemwagikia juu yake kimezungumziwa kana kwamba kilikuwa kichafu kimaumbile

kinachoweza kunywewa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "waweza kunywa"

cha mzoga

"cha maiti"

Ni lazima kivunjwevunjwe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Ni lazima ukivunje vipandevipand"e au "Yakupasa kukisambaratisha"

Leviticus 11:36

Taariifa kwa Ujumla

Yahweh anaendele kuwaambia Musa na Aroni ni wanyama gani ambao watu waahesabu najisi

Chemchemi au kisima...patabaki kuwa safi

Maji yale ambayo watu wameruhusiwa kunywa kutoka chemchemi au kisima yanapokusanyika pamezungumziwa kana kwamba palikuwa safi kimaumbile.

kisima cha maji ya kunywa yanapokusanyika

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Kisima kinachokusanya maji ya kunywa"

mzoga wa mnyama aliye najisi

maiti ya mnyama ambaye Mungu amamtaja kuwa hafai kwa watu kumgusa au kumla amezungumziwa kana kwamba alikuwa mchafu kimaumbile

yeye atakuwa najisi

Yule mtu asiyekubalika kwa kusudi la Mungu kwa sababu kagusa mzogo wa mmojawapo wa wanyama amazungumziwa kana kwamba alikuwa mchafu kimaumbile.

mbegu...kwa ajili ya kupanda

"mbugu ambazo mnatarajia kupanda"

Mbegu hizo zitakuwa bado zingali safi...zitakuwa najisi

Mbegu ambazo Mungu amezitaja kuwa zimekubalika kwa watu kupanda zimezungumziwa kana kwamba zilikuwa safi kimaumbile na zile ambazo hazikubaki zimezungumziwa kana kwamba zilikuwa chafu

Lakini kama maji yanawekwa juu ya mbegu

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. "Lakini kama mtaweka juu ya mbengu"

Leviticus 11:39

naye yeyote amgusaye atakuwa najisi hata jioni

Tazama maelezo ya sura ya 11:31

Hata jioni

Hata machweo

Leviticus 11:41

atakua chukizo

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yapasa mmchukie" au "yapasa mkatae"

Taariifa kwa Ujumla

Yahweh anaendele kuwaambia Musa na Aroni ni wanyama gani ambao watu waahesabu najisi

hatakuwa wa kuliwa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Haipasi kumla"

watakuwa machukizo.

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yawapasa kuwachukia" au "Lazima muwakate"

Leviticus 11:43

Taariifa kwa Ujumla

Yahweh anaendele kuwaambia Musa na Aroni ni wanyama gani ambao watu waahesabu najisi

Msijitie unajisi... msije mkachafuliwa navyo.

Yahweh anarudia wazo lilelile mara mbili ili kutia nguvu amri kwamba haiwapasi kula mnyama yeyote aliyenajisi.

msijitie unasi kwavyo

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "kiasi kwamba mnakosa kuwa safi kwa sababu ya hivyo"

Leviticus 11:46

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anamaliza kuwaambia Musa na Aroni kile anachowaruhusu watu kula na kilea nachowakataza kula.

kwa jili ya kile kinachopaswa kutofautishwa kati

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. :"kwa ajili ya kupambanua baina ya"

kutofautishwa kati ya kilicho najisi na kilicho safi

Wale wanyama ambao MUngu aliwataja kuwa hawafai kwa watu kuwa gusa au kuwala wamezungumziwa kana kwamba walikuwa wachafu kimaumbile, nwa wale aliowataja kukubalika kwa watu kuwagusa na kuwala wamezungumziwa kana kwamba walikuwa wasafi kimaumbile.

ambavyo vyaweza...visivyoweza kuliwa."

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ambacho mwaeza kula...amcho hamwezi kula"

Leviticus 12

Leviticus 12:1

naye atakuwa najisi

Mwanamke ambaye watu wengine haiwapasi kumgusa kwa sababu anatokwa ujauzito wake anazungumziwa kana kwamba alikuwa najisi kimaumbile.

katika siku za kipindi chake kwa mwezi

Hii hurejealea kipindi cha mwezi mwanamke anapotokwa na kutokana na ujauzito wake.

nyama ya govi la mtoto mvulana itatahiriwa

Ni kuhani tu pekee angeweza kufanya tendo hili. Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "kuhani ndiye apaswaye kumtahiri mtoto mvulana"

Leviticus 12:4

utakaso wa mama wa kutokwa damu yake utaendelea kwa muda wa siku thelathini na tatu

Siku tatu - Hii humaanisha kwmba mama atabakia najisi kwa siku sitini na tatu.

muda wa thelathini na tatu

siku tatu - "siku 33"

naye atakuwa najisi kwa muda wa majuma mawili

Mwanamke ambaye watu wengiine haiwapasi kumgusa kwa sababu anatokwa damu kutokana na mimba yake amezungumziwa kana kwamba alikuwa mchafu kimaumbile.

kwa mud wa majuma mawili

"kwa siku 14"

wakati wa kipindi chake

Tazama maelezo ya sura ya 12:1

siku sitini na sita

siku sita - "siku 66"

Leviticus 12:6

Siku za kutakaswa kwake zitakapomalizika

Siku za mwezi za utakaso wake zitakapokamilika"

kwa ajili ya mwana au bint

Hii hurejelea idadi tofauti ya siku za utakaso kutegemeana na jinsia ya mtoto anayemzaa; mwana au binti.

Leviticus 12:7

naye atatakaswa kutokana kutiririka kwa damu yake

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "na hili litamtakasa kutoka katika kutokwa na damu kwake kunaoendelea wakati wa kuzaliwa kwa mtoto.

kama hana uwezo wa kutoa mwana-kondoo

Fasiri sentensi hii ili kuweka wazi kutokuweza kwa mwanamke kununua dhabihu ya mnyama. : "Iwapo hana fedha ya kutosha kukunulia mwana-kondoo"

naye atakuwa safi

Mwanamke ambaye watu wengine wangeweza kumgusa anazungumziwa kana kwamba alikuwa safi kimaumbile.

Leviticus 13

Leviticus 13:1

lazima aletwe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "kisha yapasa mmoja kumleta yeye" au "kisha yapasa yeye aende"

kwa mmoja wa wanawe

"kwa mmoja wa watoto wa Aroni"

Leviticus 13:3

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni juu ya kile watu wafanye.

ngozi ya mwili wake

"Wake" hapa humrejelea mtu mwenye ugonjwa wa ngozi.

ugonjwa wa kuambukiza

ugonjwa ambao unaweza kuenea kwa urahisi kutoka kwa mtu mmoja hadi kwa mwingine.

atamtangaza kuwa ni najisi

"ni lazima kuhani amtangaze najisi mtu huyo." Mtule yule ambaye watu wengine hawapaswi kungusa amezungumziwa kana kwamba alikuwa mchafu kimaumbile.

kwa siku saba.

"kwa siku 7"

Leviticus 13:5

huyo kuhani itambidi kumchunguza

Anayechunguzwa hapa ni yule mtu aliye na ugonjwa wa ngozi

kama haujaenea kwenye ngozi

Hii inamaanisha kwamba kama ugonjwa wa ngozi haujaongozeka katika ukubwa au haujasogea kwenye sehemu zingine za mwili.

siku ya saba

"Ya saba" ni idadi kwa 7. : "siku ya 7"

siku saba

"Siku 7"

Naye kuhani atamtangaza safi ...yeye ni safi.

Yule mtu ambaye wengine wangemgusa amezungumziwa kana kwamba ni safi kimbaumbile.

upele

Hii ili eneo la ngozi lililoumbuliwa, lakini upele upele hataenea kwa watu wengine.

Leviticus 13:7

amejionyesha

Hii hurejea moja kwa moja kwa mtu aliye na ugonjwa wa ngozi.

kuhani atamtangaza kuwa najisi

Yule mtu ambaye watu wengine haiwapasi kumgusa amezungumziwa kana kwamba alikuwa mchafu kimaumbile

ugonjwa wa kuambukiza

Tazama maelezo ya sura 13:3.

Leviticus 13:9

huyo yapasa aletwe kwa kuhani

Kuhani aliamua iwapo ugonjwa ulikuwa umesambaa. Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "mmoja nanweza kumleta kwa kuhani" au "anapaswa kumwendea kuhani"

endapo...kumekuwa na nyama mbichi kwenye uvimbe.

"Nyama mbichi" hapa inaweza kumaanisha vidonda vilivyowazi juu ya ngozi au yaweza kumaanisha ngozi mpya imemea, lakini eneeo kukizunguka badao inaugonjwa. ama mojawapo inanyesha kwamba ugonjwa wa ngozi yenye hauponi sawasawa.

ugonjwa sugu wa ngozi

Huu ni ugonjwa ambao au unapona kwa muda wakati mrefu.

naye kuhani atamtangaza kuwa najisi...yeye tayari ni najisi

Yule Mungu ambaye watu wengine hawapasi kumgusa anazungumziwa kana kwamba alikuwa mchafu kimaumbile.

Leviticus 13:12

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni yawapasayo watu kufanya mtu anapokuwa na ugonjwa wa ngozi.

kuhani atamtangaza mtu huyo...safi...naye atakuwa safi

Mtu ambaye watu wengine wanaweza kumgusa amezungumziwa kana kwamba alikuwa safi kimaumbile na mtu ambaye watu wengine haiwapasi kumgusa amezungumziwa kana kwamba alikuwa mchafu kimaumbile.

Leviticus 13:15

Kuhani atamtangaza...najisi kwa sababu hiyo nyama yake mbichi ni najisi

Tazama maelezo ya hapo juu 13:6

kumtangaza kuwa najisi

Anayetangazwa hapa ni yule mwenye ugonjwa wa ngozi

nyama mbichi

Tazama mafafanuzi yaliyo kwenye 13:9

ugonjwa wa kuambukiza

Imefasiriwa kama ilivyofanyika katia 13:3

kuhani atatangaza kwamba mtu huyo kuwa safi

Yule mtu ambaye watu wengine wanaweza kumgusa amezungumziwa kana kwamba akuwa safi kimaumbile.

Leviticus 13:18

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu inawapasa kufanya mtu anapokuwa na ugojwa wa ngozi.

Jipu

Eneo juu ya ngozi iliyoambukizwa lenye maumivu makali.

yapasa kuonyeshwa kwa kuhani.

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yapasa alionyeshe kwa kuhani"

kuhani atamtangaza kuwa najisi

Mtu ambaye watu wengine haiwapasi kumgusa amezungumzwa kana kwamba alikuwa mchafu kimaumbile.

Leviticus 13:21

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu inawapasa kufanya mtu anapokuwa na ugojwa wa ngozi.

analichunguza

Kinachochunguzwa hapa ni ule uvimbe au doa ling'aalo juu ya ngozi.

kuhani atamtangaza kuwa najisi.

Tazama maelezo ya sura ya 13:20

naye kuhani atamtangaza kuwa safi

Mtu ambaye watu wengine wanaweza kumgusa amezungumziwa kana kwamba alikuwa safi kimaumbile.

Leviticus 13:24

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu inawapasa kufanya mtu anapokuwa na ugojwa wa ngozi.

Ugonjwa wa kuambukiza

Tazama maelezo sura ya 13:3

naye kuhani atamtangaza kuwa najisi

Tazama maelezo ya sura 13:20

Leviticus 13:26

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu inawapasa kufanya mtu anapokuwa na ugojwa wa ngozi.

analichunguza

Kinachochunguzwa hapa ni lile jeraha la moto juu ya ngozi ya mtu.

naye kuhani atamtangaza kuwa najisi

Tazama amaelezo ya sura 13:20

Ugonjwa wa kuambukiza

Tazama maelezo ya sura 13:3

, naye kuhani atamtangaza kuwa safi

Tazama maelezo ya sura 13:23

Leviticus 13:29

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu inawapasa kufanya mtu anapokuwa na ugojwa wa ngozi.

kuhani atamtangaza kuwa najisi

Tazama maelezo ya sura 13:20

Leviticus 13:31

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu inawapasa kufanya mtu anapokuwa na ugojwa wa ngozi.

Leviticus 13:32

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu inawapasa kufanya mtu anapokuwa na ugojwa wa ngozi.

basi, yapasa mtu huyo kunyolewa., lakini sehemu yenye ugonjwa haitanyolewa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "mtu huyo atalazimika kunyoa nywele zilizokaribu na jipu lakini siyo zile nywele zilizojuu ya jipu"

Leviticus 13:34

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu inawapasa kufanya mtu anapokuwa na ugojwa wa ngozi.

ule ugonjwa

"Ugonjwa" hapa humaanisha ule ugonjwa juu ya kichwa au kidevu cha mtu.

kuhani atamtangaza kuwa safi. Mtu huyo yapasa kufua nguo zake, na kisha atakuwa safi

Tazama maelezo ya sura 13:23

Leviticus 13:35

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu inawapasa kufanya mtu anapokuwa na ugojwa wa ngozi.

baada ya kuhani kutangaza kuwa alikuwa safi...Yeye ni safi, naye kuhani atamtangaza safi

Tazama maelezo ya sura 13:23

Mtu huyo ni najisi

Tazama maelezo ya sura 13:20

Leviticus 13:38

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu inawapasa kufanya mtu anapokuwa na ugojwa wa ngozi.

meupe kwa kufifia

kovu jeupe

Kovu

Tazama maelezo ya 13:5

Yeye yu safi.

"Mtu huyo yu safi"

Yeye yu safi.

Tazama maelezo ya sura 13:23

Leviticus 13:40

aelezo kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu inawapasa kufanya mtu anapokuwa na ugojwa wa ngozi.

yeye yu safi

Tazama maelezo ya sura 13:23

Leviticus 13:42

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu inawapasa kufanya mtu anapokuwa na ugojwa wa ngozi.

Ugonjwa wa kuambukiza

Tazama maelezo ya sura 13:3

naye ni najisi...atamtangaza kuwa najisi

Tazama maelezo ya sura 13:20

Leviticus 13:45

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu inawapasa kufanya mtu anapokuwa na ugojwa wa ngozi.

nje ya kambi

Kambi ni eneo ambao Waisraeli wengi wailiishi. Mtu najisi alikuwa haruhusiwi kuishi miongoni mwao kwa sababu ugonjwa wake unaweza kuenea kwa wengine.

Najisi, najisi

Tazama aelezo ya sura 13:20

Leviticus 13:47

vazi la mtu huchafuliwa na ukungu

"Vazi lenye ukungu juu yake" au Vazi ambalo linaukungu"

kuchafuliwa

Kuwa chafu kwa sababukitu fulani chenye madhara kimeongezwa kwake.

ukungu

Kuvu, mala kwa mara huwa na rangi nyeupe, ambayo hukua juu ya vitu vilivyovichafu au vyenye unyevunyevu

au kitu chochote kilichosukwa au kufu

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji' : : "au kitu chochote ambacho mtu aliye amekisokota au kukisuka"

Iwapo sehemu iliyochafuliwa ina rangi ya kijani au nyekundu katika vazi

"kama kuna uchafu wa kijani au wenye wekundo kwenye vazi"

kitu chochote kilichotengenezwa kwa ngozi

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "kitu chochote kile ambacho mtu amekitengeneza kutoka na na ngozi"

lazima kionyeshwe kwa kuhani

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Mmiliki wake yapasa kukionyesha kwa kuhani"

Leviticus 13:50

siku saba

Tazama maelezo ya sura 13:5

siku ya saba

Tazama maelezo ya sura 13:6

kitu chochote ambacho ngozi imetumika

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "kitu chochote ambacho mtu anatumia ngozi"

kifaa chochote kilichoonekana na ukungu ndani yake

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Chochote ambacho kinapatika na ukungu wenye kudhuru juu yake"

kifaa hicho ni najisi

Maelezo yake yaweza kufanana na ya sura 13:20

huo ukungu unaweza kusababisha ugonjwa

Huo ukungu wenyekudhuru waweza kusababisha ugonjwa ndani ya mtu anayekikaribia kifaa.

Chombo hicho lazima kiteketezwe kabisa kwa moto

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yapasa akiteketeze hicho chombo kabisakabisa

Leviticus 13:53

basi atawaamru

"kisha kuhani atamwamru mmiliki" Hapa kuhani anawaambia watu namna ya kuvitendea vyombo vya nymbani ambavyo yamkini vilikuwa vimembukizwa.

hicho kifaa kilichopatikana na ukungu

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ambamo wamegundua mna ukungu"

baada ya kuwa kimesafishwa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "baada ya kukiosha kifaa"

kifaa hicho ni najisi

Kitu ambacho Mungu amekitangaza kuwa hakifai kwa watu kukigusa kimezungumziwa kana kwamba kilikuwa kichafu kimaumbile.

Yapasa ukichome kifaa hicho

"ukichome" hapa haimaanishi kuhani hasa. Inamaanisha tu mtu impasaye kukichoma kifaa.

Leviticus 13:56

baada ya kuwa umeoshwa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Baada ya miliki kuwa amekiosha"

lazima utakichoma moto

Anayelazimika hapa haimaanishi kuhani hasa. bali inamaanisha tu yule anayepaswa kukichoma hicho chombo.

iwapo unakisafisha kifaa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : Endapo mmiliki anakiosha"

nao ukungu ukawa umetoka, nacho kifaa lazima kisafishwe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "kisha huyo mmiliki lazima akioshe"

kisha kitakuwa safi.

Tazama maelezo ya sura 13:23

Leviticus 13:59

ukungu katika vazi....lilotengenezwa kwa ngozi

Tazama linavyofasireiwa katika sura 13:47

ili kwamba mweze kuvitangaza

"ili kwamba kuhani aweze kukitangaza"

safi au najisi

Tazama maelezo ya sura 13:20-23

Leviticus 14

Leviticus 14:1

Maelezo kwa Ujumla

Yahweh aHii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji.nawaambia Musa na Aroni kile ambacho watu wanapaswa kufanya mtu anapotakaswa ugonjwa wa ngozi.

siku yake ya utakaso

Hii hurejelea siku ya ambayo kuhani anamtangaza mtu kuwa ni safi kwa kanuni za kidini

Ni lazima aletwe kwa kuhani

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Mtu mmoja anaweza kumleta kwa k"uhani au "Yeye anaweza kwenda kwa kuhani"

Leviticus 14:3

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendele kuwaambia Musa na Aroni ambacho watu wafanye mtu anapotakaswa ugonjwa wake wa ngozi.

madhara ya ugonjwa wa ngozi

Tazama maelezo ya sura ya 13:3

mtu wa kutakaswa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Mtu anayemtakasa"

ndege safi

Tazama maelezo ya sura ya 13:23

kitani nyekundu

"uzi mwekundo"

Leviticus 14:6

Taarifa kwa Ujumla

Tazama maelezo ya sura 14:3

ndege aliyechinjiwa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Ndenge ambaye mtu alimuua"

mtu ambaye amekuwa akitakaswa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "mtu anayemtakasa"

atamtangaza kuwa safi

Tazama maelezo ya sura 13:23

Leviticus 14:8

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anawaambia Musa na Aroni kile ambacho watu wafanye mtu anapotakaswa ugonjwa wa ngozi

ambaye amekuwa akitakasw

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Mtu ambaye kuhani anamtakasa"

naye atakuwa safi

Tazama maelezo ya sura 13:23

Leviticus 14:10

itambidi kuchukua

Hapa anayepaswa kuchukua ni yule aliyetakaswa.

efa

Efa moja ni sawasawa na lita 22.

logi

Logi moja ni sawasawa na lita 0.31

yeye atakaswaye

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "mtu anayemtakasa"

Leviticus 14:12

Logi

Logi mmoja ni sawasawa na lita 0.31

katika eneo la hema

Kirai hiki kinafafanua kirai kilichotangulia na kutoa maelezo zaidi juu ama kuhani aliyekuwa amchinje huyo mwana-kondoo

Leviticus 14:14

mtu wa kutakaswa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "mtu anayemtakasa"

Logi

Logi moja ni sawasawa na lita 0.31

kunyunyiza sehemu ya mafuta...mbele za Yahweh.

"kunyunyizia sehemu ya mafuta... mbele za Yahweh" hakuna kiashiria cha kile ambacho kuhani alinyinyizia mafuta juu yake.

Leviticus 14:17

mafuta yaliyobaki mkononi mwake

"mafuta yaliyobaki yaliyomo mkononi mwake

Mtu anayetakaswa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : " mtu anayemtakasa"

mbele za Yahweh

"katika uwepo wa Yahweh"

Leviticus 14:19

yake yeye wa kutakaswa

Hii yaweza kufasiriwe katika mtindo wa utendaji. : "mtu anayemtakasa"

naye atakuwa safi

Tazama maelezo ya sura 13:23

Leviticus 14:21

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu wanapaswa kufanya mtu anapotakaswa ugonjwa wa ngozi.

hawezi kumudu

"hana fedha ya kutosha kununua"

kutikiswa...kwa ajili yake

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ambaye kuhani atamtikisa...kwa ajili ywke"

moja ya kumi ya efa

kumi ya efa ni - moja ya kumi ya efa ni swaswa na lita 22.

Logi

Logi moja ni swasawa na lita 0.31

Leviticus 14:24

Logi

Logi moja ni swasawa na lita 0.31

anayemtakasa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yule anayemtakasa"

Leviticus 14:26

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kile ambacho watu wanapaswa kufanya mtu anapotakaswa ugonjwa wa ngozi.

sehemu ya mafuta...atanyunyizia...mbele za Yahweh

"sehemu ya mafuta...nyunyizia...mbele za Yahweh." Hakuna kiashiria cha kile ambacho kuhani aliyanyunyizia mafuta juu yake.

Leviticus 14:28

yule wa kutakaswa

Tazama maelezo ya sura 14:19

Leviticus 14:30

Atatoa

"Kuhani atatoa"

yule wa kutakaswa

Tazama ameleo ya sura 14:19

Ugonjwa wa kuambukiza

Tazama maelezo ya sura 13:3

asiye mudu

: "asiyekuwa na fedha ya kuutosha kuweza kununua"

Leviticus 14:33

Mtakapoingia

"mtakapoingia" hapa inamaanisha watu wa sraeli.

ukungu

Tazama maelezo ya sura 13:42

katika nchi ya milki yenu

Neno "milki" laweza kufasiriwa kama kitenzi. : "katika nchi mnayoimiliki"

Leviticus 14:36

ili kwamba kusiwe na kitu ndani ya nyumba kitakachonajisika

mara tu kuhani alipoitangaza nyumba najis, kila kitu kilichokuwa kwenye nyumba kilikuwa najisi pia. Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "kiasi kwamba hahitaji kutangaza kitu cho chote kilichosalia ndani ya nyumba kuwa najisi"

ndani ya nyumba kitakachonajisika

Tazama maelezo ya sura 13:20

katika bonde za kuta.

Hii inamaanisha kwamba kuhani ndiye atakayeamua iwapo ukungu umeingi ndani ya nyuso za kuta tu.

Leviticus 14:39

ambayo kwayo ukungu umepatikana

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ambamo ukungu liuona"

mahali palipo najisi

Tazama maelezo ya sura 13:20

Leviticus 14:41

Naye atataka

"Naye" hapa humaanisha kuhani.

zikwanguliwe kuta zote za ndani ya hiyo nyumba

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "kwamba mmiliki anazikwangua kuta zote za nadani"

vilivyochafuliwa na hivyo vifaa vilivyokwanguliwa

Hii humaanisha vifaa vyenye ukungu juu yake. Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : KIfaa kilichochafuliwa kile walichokikwangua"

mahali paliponajis

Tazama maelezo ya 13:20

mawe yaliyoondolewa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yale mawe waliyoyaondoa"

lazima watumie udongo mpya kuipiga lipu hiyo nyumba

"lazimz wayafunike hayo kwa udongo mpya"

Leviticus 14:43

katika nyumba...na kupigwa lipu upya

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "katika nyumba baada ya mmiliki kuyaondoa mawe, amezikwangua kuta, na kuyafunika mawe kwa udongo.

nyumba hiyo ni najisi

Taama maelezo ya sura 13:20

Leviticus 14:45

Yapasa hiyo nyumba ibomolewe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yapasa waiangushea nyumba chini"

Na hayo mawe, na udongo wa lipu vitachukuliwa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yapasa waondowe mawe, mbao, na lipu yote katika nyumba"

yeyote aingiaye ndani ya nyumba....atakuwa najis

Tazama maelezo ya sura ya 13:20

hata jioni

"mpaka machweo"

Leviticus 14:48

nyumba kuwa imepigwa lipu

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "mmiliki anaweka udongo mpya juu ya nyumba"

ndipo atatangaza kuwa nyumba hiyo ni safi

Tazama maelezo ya sur 13:23

Leviticus 14:49

mti wa mwerezi , hisopo, kitambaa chekundu ... damu ya ndege aliyeuawa

Tazama maelezo ya sura ya 14:3

damu ya ndege aliyeuawa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ile damu ya ndege ambaye yeye limuua"

Leviticus 14:52

Atalitakaza nyumba

"Kuhani ataifanya safi nyumba kwa kawaida za kidini"

nayo itakuwa safi

Tazama maelzo ya sura 13:23

Leviticus 14:54

athari ya ugonjwa wa ngozi

Tazama maelezo ya sura13:3

Ukungu

Tazama maelezo ya 13:47

vipele

Tazama amelezo ya sura 13:5

najisi...safi

Tama maelezo ya sura13:20 na 23

Leviticus 15

Leviticus 15:1

unaotoka mwilini mwake

Hii hurejelea semhemu nyeti za mtu.

huwa najis

Tazama maelezo ya sura 13:20

ni najisi

"mwili wake ni najisi" au "yeye ni najisi"

Leviticus 15:4

najisi

Tazama maelezozo ya sura 13:20

Yeyote agusaye kitanda....na atakuwa najisi

Tazama maelezo ya sura ya 13:23

Hata jioni

Mpaka machweo.

Leviticus 15:6

naye atakuwa najisi

Tazama maelezo ya sura 13:20

hata jioni

"paka machweo"

agusaye mwili

"yeye agusaye sehemu yoyote ya mwaili"

Leviticus 15:8

mtu mwingine aliyesafi

Tazama maelezo ya sura 13:23

atakuwa najisi

Tazama maelezo 13:20

Tandiko

Tandiko ni kiti cha ngozi ambacho mtu hukiweka mgongoni mwa farasi ili kumpanda aende safari

Tandiko lolote...litakuwa najisi

Tazama maelezo ya sura 13:20

Leviticus 15:10

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwaambia Musa na Aroni kiwapasacho watu kutenda ili kuzuia maabukuizi.

mtu huyo

Hii humrejelea mtu aliye maambukizi ya ugiligili.

atakuwa najisi

Tanzama maelezo ya sura 13:20

hata jioni

"mpaka macheo"

Yeyote yule aliye na mtiririko kama huo anamgusa

Yeyote aguswaye na mtu mwenye mtiririko"

Chungu chochote cha udongo anachokigusa mwenye kutiririkwa na ugiligili kama huo yapasa kivunjwe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Mtu yeyote anaweza kuweza kukuvunja chungu chochote cha udongo ambacho amekigusa mtu mwenye mtirirko kama huo"

kila chombo cha mti lazima kisafishwe kwenye maji

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ni lazima mtu asuuze kwenye maji kila chombo cha mbao"

Leviticus 15:13

anapotakaswa kutoka kwnye kutiririkwa kwake

Tazama maelezo ya sura 13:23. Na hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "aponapo kutka kwenye kutiririka kwake"

Naye atakuwa safi

Tazama maelezo ya sura 13:23

Leviticus 15:16

najisi hata jioni

Tazama amelezo ya 13:20

hata jioni

"mpaka macheo"

Kila vazi...lazama ifuliwe kwa maji

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Mtu atalazimika kufua kila vazi au ngozi ambayo juu yake kuna shahawa

Leviticus 15:19

hedhi...kipindi chake

Haya yote mawili hurejelea kwenye kipindi cha kutirirka kwa damu kutoka kwenye tumbo la mwanamke.

uchafu kutengwa kwake kutaendelea

"ataendelea kuwa mchafu"

kitakuwa najisi

Yazama maelezo ya sura 13:20

Leviticus 15:21

Kitanda chake

Hii humrejelea mwanamke aliyeingia damuni"

mtu huyo atakuwa najisi

Tazama maelezo ya sura 13:23

Hata jioni

"mpaka macheo"

Leviticus 15:24

uchafu wake utiririkao

"mtirirkiko wake najisi" au "damu yake itokayo kwenye mji wa mimba"

atakuwa najisi

Tazama maelezo ya sura 13:20

Leviticus 15:25

atakuwa kama alivyokuwa kwenye siku zake za hedhi

Hii humaanisha kwamba mwanamke atokwaye damu kutoka kwenye mji wake wa mimba wakati mwingine wowote badala ya ule wa hedhi yake ya kawaida, yeye bado ni najisi kama tu wakati wa hedhi yake.

Yeye ni najisi...yeyote amgusaye...atakuwa najisi

Tazama maelezo ya sura 13:20

a kila kitu akaacho juu yake kitakuwa najisi

Tazama maelezo ya sura 13:20

Leviticus 15:28

Lakini yeye

Neno "yeye" humaanisha mwanamke aliyedamuni"

ametakaswa kutoka kwenye kutokwa na damu kwake

kwa maelezo ta awali tazama 13:23. Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. "aponapo kutoka kwenye kutirirkwa kwake kwa damu"

atakuwa safi

Tazama maelezo ya sura 13:23

atajitwalia

"atachuku kwa ajili yake mwenyewe"

unajisi wa wake wa kutokwa na damu

"mtirirko wake wa damu umfanyao yeye najis"i

Leviticus 15:31

Hivi ndivyo inavyokupasa kuwatenga watu wa Israeli kutoka katika unajisi wao

Yahweh anazungumzia juu ya kuwalinda watu dhidi ya kuwa najisi kana kwamba ilikuwa ni kuwaweka watu salama mbali kutoka kwenye uchafu. "Hivi ndivyo iwapasavyo kuwakinga watu wa Israeli dhidi ya kuwa najisi"

unajisi wao

Tazama maelezo ya sura ya 13;@0

Leviticus 15:32

Hizi ndizo kanuni

"haya ndiyo mambo yapasayo kutendeka"

kumfanya najisi...humfanya najisi

Tazama maelezo ya sura 13:20

aliye katika kipindi cha hedh

"aliyedamuni" au "ananyetokwa damu kutoka kwenye mji wake wa mimba"

Leviticus 16

Leviticus 16:1

Aroni wanwanawe

Hii huwarejelea Nadabu na Abihu. Walikufa kwa sababu walileta kwa Yahweh moto ambao hakuukubali. (Tazama 10:1)

Leviticus 16:3

Hapa ndipo impasapo

"Hivi ndivyo"

kanzu yake ya ndani ya kitani

"Vazi la ndani." Hii ni nguo iliyovaliwa yapili kutoka kwenye ngozi chini ya nguo za nje.

mshipi

Kipande cha nguo ambacho hufungwa kuzunguka kiuno kifua

kilemba

kipande cha nguo ambacho hungwa kuzunguka kiuno au kifua

kutoka kwenye kusanyiko

Hiki ni kifuniko cha kichwani kilichofnywa kutoka na vitambaa vya nguo vilivyoringishwa

kutoka kwenye kusanyiko

"kutoka kwenye mkutano wa watu"

Leviticus 16:6

sadaka ya dhambi, ambayo itakuwa kwa ajili yake mwenyewe,

"sadaaka ya dhambi kwa ajili yake"

Leviticus 16:8

Mbuzi wa azazeli

"yule mbuzi anayepelekwa mbali." iAroni alitakiwa kuwa na mtu wa kumwacha huru huyo mbuzi aende nyikani.

kura imemwangukia

"yule ambaye kura imeteuliwa"

Lakini mbuzi...lazima aletwe mbele za Yahweh

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Aroni atamleta huyo mbuuzi...mbele za Yahweh akiwa hai.

Leviticus 16:11

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa kile ambacho Aroni anapaswa kufanya siku ile ya upatanisho.

amchinje huyo fahali

Aroni angeikusanya damu ya fahali kwenye bakuli ili kwamba baadaye ainyunyize juu ya kiduniko cha upatanisho. Maana kamili ya maelezo haya yaweza kuwekwa wazi.

Leviticus 16:12

chetezo

chombo kilichokuwa ajili ya moto na ubani, kilitumiwa na makuhani.

ubani...wenye harufu ya kupendeza

"ubani ulinukia vizuri." Hii ilimaanisha harufu na siyo ladha ya ubani.

Leviticus 16:14

damu ya fahali

Tazama maelezo ya sura 16:11

kuinyunyiza kwa kidole chake

Alitumia kidole chake kurushia damu

upande wa mbele wa kifuniko cha upatanisho

Aliiweka hiyo damu upande wa juu wa kifuniko. pia aliiweka upande wa pembeni mwa kifuniko uliomwelekea alipoingia eneo la patakatifu pa patakatifu

mbele za kifuniko cha upatanisho

Maana zinazo wezekani ni 1) "chini ya kifuniko cha upatanisho kenye sanduku" au 2) ardhini chini ya mbele ya kifuniko cha upatanisho."

Leviticus 16:15

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa kile ambacho Aroni anapaswa kufanya siku ile ya upatanisho.

lazima ainyunyize juu ya kifuniko cha upatanisho na mbele ya kifunuko cha upatanisho

Tazama maelezo ya sura 16:14

Naye atafanya upatanisho kwa ajili ya mahali patakatifu kwa sababu ya matendo ya unajisi ya watu wa Israeli

Tahambi za watu wa Israeli zilipanajisi patakatifu.

matendo ya unajisi...uasi...dhambi

Maneno haya kimsingi ni yale yale. Nayasisitiza kwamba watu wametenda aina zote za dhambi.

Matendo ya unajisi

Tazama amelezo ya sura 13:20

katika uwepo wa matendo yao ya unajisi.

Kile kirai "matendo yao ya unajisi" huwakilisha watu wafanyao matendo ya dhambi. : "katika uwepo wa watu wafanyao matendo ya dhambi"

Leviticus 16:17

Yapasa atoke kwenda nje na kwenda kwenye madhabahu hapo mbele za Yahweh

Hii ni madhabahu ya dhabihu iliyo ndani ya uwanda wa hema

kufanya upatanisho kwa ajili ya hiyo

Kama lilivyo eneo la hema la kukutania, madhabahu nayo ni najisi kwa sababu ya dhambi za watu.

pembe za madhabahu

Tazama maelzo ya sura 4:6

ili kuitakasa

Tazama maelezo ya sura 13:23

kuitenga kwa ajili ya Yahweh, mbali na matendo ya unajisi ya watu wa Israeli.

Madhabahu kuwa imetengwa kwa imezungumziwa kana kwamba ilikuwa imetengwa na dhambi za watu kimaumbile

matendo ya unajisi

Tazama maelezo ya sura 13:20

Leviticus 16:20

lazima atamleata huyo mbuzi aliyehai

Mbuzi hyu anaitwa wa azazeli katika 16:8

kukiri juu yak

"kukiri juu ya mbuzi"

ataweka hizo dhambi juu ya kichwa cha huyo mbuzi

Hapa matendoya Aroni yalikuwa ishara ya uhamisho wa dhambi za watu kwenda kwa mbuzi kama ishara kwamba huyo mbuzi angebeba adhabu kwa ajili ya hatia yao.

maovu...uasi...dhambi

Haya yote kimsingi yanamaanisha jambo moja. Aroni anaungama kila aina ya dhambi watu waliyoitenda.

Leviticus 16:23

na kuvua mavazi ya kitani

Haya yalikuwa mavazi maalum aliyovaa Aroni pekee alipoingi patakatifu pa patakatifu.

Yapasa aoge mwili wake kwa maji mahali patakatifu

"Mahali Pataktifu" haimaanishi kwenye hema la kukutania. Hili lilikuwa ni eneo tofauti lililotengwa kwa ajili yake kuoga humo.

kuvaa nguo zake za kawaida

Haya ni mavazi ambayo Aroni alivaa kwa ajili ya majukumu yake ya kawaida.

Leviticus 16:25

Naye yapasa kuyatekeza

"Aroni yapasa yateketeze"

Huyu mtu anayemwachia mbuzi wa azazeli huru, lazima afue nguo zake na kuoga mwili wake katika maji

Mtu huyu alikuwa najisi kwa sababu kugusana na na huyo mbuzi wa azazeli, aliyebeba dhambi ya watu.

mbuzi wa azazeli

Tazama maelezo ya sura 16:8

Leviticus 16:27

ambaye damu yake ililetwa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ambaye damu yake Aroni aliileta"

lazima wapelekwe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yapasa mtu fulani ambebe"

ngozi zao

"ngozi zao" "zao" hapa humaanibsha fahali na mbuzi

Leviticus 16:29

kwa ajili yenu

Neno "yenu" humaanisha watu wa Israeli.

katika mwezi wa saba, siku ya kumi ya mwezi,

Huu ni mwezi wa saba wa kalenda ya Kiebrania. Siku ya kumi ni karibu na mwisho wa mwezi wa septemba kwenye kalenda ya kimagharibi.

upatanisho utafanywa kwa ajili yenu

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Aroni atafanya upatanisho kwa ajili yenu"

kuwatakasa ninyi...ili muwe safi

Tazama maelezo ya sura ya 13:23

kwa ajili ya kusanyiko la watu.

"kwa ajili ya watu wote wa Israeli"

Leviticus 16:32

ambaye atapakwa mafuta na kuwekwa wakfu

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "watakayempaka mafuta na kumweka wakfu.

katika nafasi ya baba yake

Kuhani mkuu alipokufa , mmoja wa wanawe angechukua nafasi yake.

mavazi matakatifu

Hizi ni nguo maalum alizopaswa kuzivaa kuhani mkuu alipoingia mahali patakatifu pa patakatifu

kwa ajili ya kusanyiko la watu.

"kwa ajili ya watu wote wa Israeli"

Leviticus 16:34

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anamaliza kumwambia Aroni kile ambacho watu yawapasa kufanya.

Hili lilifanyika kama Yahweh alivyomwamuru Musa.

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utengaji. : "Naye Musa akafanya kama alivyoamru Yahweh" au "Naye Aroni akafanya kama Yahweh alivyomwamru Musa"

Leviticus 17

Leviticus 17:1

mbele za hema

"mbele za hema la Yahweh"

mtu huyo ni sharti akatiliwe mabali kutoka miongoni mwa watu wake

Tazama amelezo ya sura 7:19. : "mtu huyo yawezekana asiishi miongoni mwa watu wke" au yapasa mmtenge mtu huyo na watu wake"

Leviticus 17:5

kwa kuhani ziweze kutolewa kuwa sadaka

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "kwa kuhani ili kwamba aweze kuwatoa dhabihu"

Leviticus 17:7

ambazo kwazo hutenda kama makahaba

Watu ambao wamekuwa siyo waaminifu kwa Yahweh kwa kuabudu miungu ya uongo wamezungumziwa kana kwamba walikuwa akitenda kama mwanaume anayemsaliti mkewe kwa kufanya uzinzi. : "ambayo kwa ajili yake siyo waaminifu kwa Yahweh"

Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yao katika vizazi vya watu wao vyote

Tazama maelezo ya sura 3:15

Leviticus 17:8

mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali kutoka kwa watu wake

Tazama maelezo ya sura 7:19 na ya suara 17:4

Leviticus 17:10

Nitaukaza uso wangu dhidi ya mtu huyo

Neno "uso" huwakilisha nafsi. Nahu hii humaanisha kumkataa mtu au kitu fulani. : "Nitakuwa nyume na mtu huyo" au "nitamkataa mtu huyo" au "Nitamkataa huyu mtu"

kumkatilia mbali atoke miongoni mwa watu wake

Mtu aliyeondolewa kwenye jamii yake anazungumziwa kana kwamba amekatwa kwa watu wake, kama mtu akatavyo tawi kutoka kwenye mti. : "Sitamruhusu mtu huyu aendelee kuishi miongoni mwa watu wake tena"au "Nitamtenga mtu huyo kutoka kwa watu wake"

Kwa kuwa uhai wa mnyama yeyote umo katika damu yake...ipatanishayo kwa ajili ya uhai

Hii humaanisha MUngu huitumia damu kupatanisha kwa ajili ya dhambi za watu kwa sababu damu ni uhai. Watu wasinywe damu kwa sanbabu ina kusudi hili maalum.

Leviticus 17:12

Niliwaambia

"Niliwambia" hapa humaanisha Yahweh

asiwepo miongoni mwenu impasaye kula damu

"asiwepo mingoni mwenu awezaye kula nyama pamoja na damu ndani yake"

awezaye kuliwa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ambao nilisemba wanaweza kuwala"

na kuifukia kwa udongo hiyo damu

"na kuifunika damu mavumbi"

Leviticus 17:14

uhai wa kila kiumbe umo katika damu yake

Hii humaanisha kwamba damu ndiyo ikiwezeshayo kiumbe kuishi. Maana kamili ya kauli hii yaweza kufanywa wazi. "kila kiumbe chaweza kuishi kwa sababu ya damu yake"

Yeyote ailaye ni lazima akatiliwe

Mtu aliyeondolewa kwa jamii yake anazungumziwa kana kwamba amekwisha kukatwa kutoka kwa watu wake, kama vile mtu angeweza kipande cha nguo au tawi la mti kutoka kwenye mti. : "yeyote alaye damu hataweza kuishi tena miongoni mwa watu wake" au "yeyote alaye damu sharti mmtenge na watu wake"

Leviticus 17:15

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuzungumza.

ambaye amelaruliwa na wanyama pori

Mnyama anayeuawa na wanyama pori anazungumziwa kana kwamba hao wanya pori wamchana vipande vipande huyo mnyama. Hii yaweza katika mtindo wa utendaji. : ""yule ambaye wanyamapori wamemuua"

ni mwenyeji wa kuzaliwa

"ni Mwisraeli"

naye atakuwa...Kisha ndipo atakuwa safi

Tazama maelezo ya 13:20 na 23

Hata Jioni

"mpaka macheo"

sharti yeye aichukue hatia yake

Hatia ya mtu imezungumziwa kana kwamba ilikuwa kitu ambacho mtu hukibeba. Neno "hatia" hapa huwakilisha adhabu kwa hatia hiyo. : "Hivyo anawajibika kwa hatia yake mwenyewe" au "kisha nitamwadhibu yeye kwa ajili ya dhambi yake"

Leviticus 18

Leviticus 18:1

Yahweh

Hili ni jina Mungu ambalo alimwambia Musa kwenye kicha kilichowaka moto. Mungu alisema kwamba hili ndilo lilikuwa jina lake milele.

Musa

Musa alikuwa nabii na kiongozi wa watu wa Waisraeli kwa zaidi ya miaka 40.

Alipokuwa mtoto, wazazi wake Musa, walimweka yeye kwenye kikapu cha mianzi ya Mto Nile ili kumficha kwa Farao wa Misri. Dada yake Miriamu dada yake Musa, Alimwangalia yeye huko. Maisha ya Musa yaliokolewa tu binti alipomwona na kumchukua kwenda naye Ikulu ili kumlea kama mwanae.

Mungu alimchagua Musa kuwaweka huru Waisraeli kutoka utumwani Misri na kuwaongoza kwenda katika Nchi ya Ahadi.

Baada ya kutoka kwa Waisraeli Misri na walipokuwa wangali wakizunguka jangwani, Mungu alimpa Musa mbao mbili za mawe zilioandikwa Amri Kumi juu yake.

Karibu kabisa na mwisho wa maisha yake, Musa aliiona tu Nchi ya Ahadi, lakini haingia kuishi humo kwa sababu hakumtii Mungu.

Kikundi cha watu, watu, watu wa,

Ule usemi "watu" au "vikundi vya watu" humaanisha vikundi vya watu wanaoshiriki lugha na utamaduni mmoja. Kile kirai "watu wa" mara kwa mara humaanisha kusanyanika la watu katika eneo fulani au katika tukio maalum.

Mungu anapotenga "kikundi cha watu" kwa ajili yake, humaanisha alichagua watu fulani ili wawe wake na kumtumikia yeye.

Katika nyakiti za Biblia, washirika wa kikundi cha watu kwa kawaida walikuwa na wazazi au mababu wamoja na waliishi mahali pamoja katika taifa au eneo maalum la nchi.

Kwa utegemeana na muktadha, kirai kama vile "watu wako" chaweza kumaanisaha "kikundi cha watu wako" au "famikia yako" au "jamaa zako."

Ule usemo "watu" mara kwa mara limetumika kumaanisha vikundi vyote vya watu juu ya nchi." Wakati mwingine zaidi lilimaanisha hasa kwa watu wasio Waisraeli au wasiomtumikia Yahweh. Katika tafasiri zingine za kiingereza ule msemo "mataifa" pia umetumika katika njia hii.

MAPENDAKEZO YA UFASIRI. Ule msemo "kikundi cha watu" waweza kufasiriwa kwa neno au kirai chenye kumaanisha, "kundi kubwa la kifamilia" au "ukoo" au "kikundi cha kikabila."

Kirai kama vile "watu wangu" chaweza kufasiriwa kama "jamaa zangu" au "Waisraeli wenzangu" au "familia yangu" au "watu wa kikundi changu," kutegemeana na muktadha.

Yale maelezo "nitawatawanya miongoni mwa watu" pia yaweza kufasiriwa "nitasababisha kwenda na kuishi pamoja na vikundi mbali mbali vya watu wengi" au "sababisha kutengana ninyi kwa ninyi na kwenda kuishi katika mikoa mingi tofauti ya ulimwengu.

Ule msemo "watu" waweza kufasiriwa "watu ulimwenguni" au "vikundi vya watu," kutegemeana na muktadha.

Kile kirai "watu wa" chaweza kufasiriw kama, "kila mmoja aishie katika" au "watu wa kutoka uzao wa" au "familia ya," kutegeana na ama linafuatiwa na jina la mahali au mtu.

"watu wote wa ulimwengu" yaweza kufasiriwa kama, "kila nafsi ulimwenguni" au "watu wote."

Kile kirai "watu" pia chaweza kufasiriwa kama "kikundi cha watu" au "watu fulani" au "kikundi cha watu" au "jamii ya watu" au "familia ya watu"

Israeli, Waisraeli, taifa la Israeli

Ule msemo "Israeli" ni jina ambalo Mungu alimpa Yakobo. Humaanisha, "yeye hushindana na Mungu."

Wazao wa Yakobo walikuja kujulikana kama "watu wa Israeli," "taifa la Israeli," au "Wasraeli." Taifa la Israeli

Mungu alitengeneza agano lake watu wa Israeli. Walikuwa watu wake wateule.

Taifa la Israeli liliundwa na makabila kumi na mbili.

Mara tu baada ya kufa kwa mfalme Sulemani, Isrseli iligawanyika katika falme mbili: Ufalme wa kusuni, uliitwa "Yuda" na ule ufalme wa kaskazini ukaitwa "Israeli."

Mara kwa mara ule msemo "Israeli" waweza kufasiriliwa kama, "watu wa Israeli" au "taifa la Israeli," kwa kutegemeana na muktatha.

Mungu

Kwenye Biblia Neno "Mungu" humaanisha nafsi ya milele aliyeumba ulimwengu pasipo kitu. Mungu huishi kama Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu. jina binafsi la Mungu ni "Yahweh" . Siku zote Mungu alikuwapo; alikuwapo kabla ya kabla ya kitu chochote kuwapo. Naye ataendelea kuwako milele

. Yeye ndiye Mungu wa kweli na ana mamlaka juu ya vitu vyote hulimwenguni.

. Mungu ni mwenye haki kwa ukamilifu, ni mwenye hakima pasipo na kikomo, mtakatifu, bila dhambi, mwenye haki, rehema, na upendo.

. Yeye ni Mungu atunzaye agano, ambaye hutimiza ahadi zake.

. Watu waliumbwa ili wamwambudu Mungu naye ndiye Yeye pekee imewapasa wao kumwabudu.

. Mungu lilifunua jina lake kuwa ni "Yahweh" ambalo humaanisha, " yeye ndiye" au "Mimi ndimi" au "Yule aliyopo (siku zote)"

. Pia Biblia hufundisha juu ya "miungu ya uongo" ambayoo ni sanamu zisizo na uhai ambayo watu huiabudu kimakosa.

MAPENDEKEZO YA UFASIRI

. Njia za kufasiri "Mungu zingejumuisha maneno kama "Uungu" au "Muumba" au "Mwenye Mamlaka yote"

. Njia zingine za kufasiri "Mungu" zaweza kuwa, "Muumbaji wa vyote" au "Bwana Mwenye mamlaka isiyo na mipaka" au "Mwenye Mamlaka yote milele."

Zingatia jinsi Mungu anavyotajwa katika lugha ya kieneo au kitaifa. Yawezekana kuwa tayari lipo neno kuhusu "Mungu" katika lugha inayotafsiriwa. Kama ndivyo, ni muhimu kuhakikisha kwamba neno hili linafaa kwa sifa baishi za Mungu wa kweli kama anavyoelezwa hapo juu.

Lugha nyingi huanza na herifu kubwa ya neno kwa Mungu aliye wa kweli ili kulitofautisha na neno kwa mungu wa uongo.

Njia nyingine ya kuonesha tofauti hizi ingetumika misemo miwili tofauti kwa "Mungu" na "muungu"

Kile kirai, "nitakuwa Mungu wao nao watakuwa atu wangu" pia chaweza kufasiriwa kama, "Mimi, Mungu, nitatawala juu ya watu nao wataniabudu mimi."

Misri, Mmisri

Misri ni taifa lililoko upande wa kaskazini mashariki mwa Africa, kusini magharibi mwa nchi ya Kanaani. Mmisri ni mtu anayetoka katika nchi ya Misri.

. Zamani za kale, Misri lilikuwa taifa lenye nguvu na tajiri.

. Misri ya zamani iligawanyika katika sehemu mbili, Misri ya chini (sehemu ya kaskazini mahali ambapo mto Nile ulitiririka kuelekea Baharini) na Misri ya juu (sehemu ya kusini). Katika Agano la Kale, sehamu hizi zilitajwa kama "Misri" na "Pathrosi" katika lugha ya asili.

Mara nyingi kilipokosekana chakula huko Kanaani, mababa wa Israeli walisafiri kwenda Misri ili kununua chakula kwa ajili aya familia zao.

Kwa muda wa mamia ya miaka, Waisraeli walikuwa watumwa huko Misri.

Yusufu na Mariamu waliterekia Misri pamoja na mtoto mchanga Yesu ili kumtoroka Herode Mkuu.

Maisha, ishi, kuishi, -wa mzima

Misemo hii yote humaanisha kuwa mzima kimaumbile, siyo mfu. Pia yametuka kiishara kumaanisha kuwa hai kiroho. Ifuatayo inazungumzia inavyomaanisha kuwa na "uhai wa kimwili" na "Uhai wa Kiroho"

MAPENDEKEZO YA UFASIRI

. Kwa utegemeana na muktadha, "maisha yaweza kufasiriwa kama "uwepo" au "nafsi" au "moyo" au "aishie" au "uzoefu"

. Ule msemo "ishi" waweza kufasiriwa "kaa" au "kuwepo."

Yale amelezo "mwisho wa maisha" yangeweza kufasiriwa kama, "alipokoma kuishi."

Yale maelezo "alitunza uhai wao" yangeweza kufasiriwa kama, "aliwaruhusu kuishi" au "hakuwaua wao."

Ule usemi "walihatarisha maisha yao" ungeweza kufasiriwa kama, "walijiweka wenyewe hatarini" au walifanya jambo fulani ambalo lingekuwa limishawaua wao."

Kifungu cha Biblia kinapozungumzia kuwa hai kiroho, "uhai"pia ungefasiriwa kama, "maisha ya kiroho" au "Uzima wa milele" kutegemeana na muktatha"

Wazo la "maisha ya kiroho" lingeweza kufasiriwa pia kama "Mungu anatufanya hai katika roho zetu" au "maisha mpya yatolewayo na Roho wa Mungu" au "kufanywa hai katika utu wetu wa ndani."

Kwa kutegemeana na muktatha, neno "-pa maisha" laweza pia kufasiriwa kama "sababisha kuwa hai" au -pa maisha mapya" au "sababisha kuishi milele."

Leviticus 18:4

Sheria zangu ndizo mtakazozitenda, na amri zangu ndizo mtakazozishika

Virai hivi viwili kimsingi humaanisha kitu kile kile na vinasisitiza kwamba ni sharti watu watii kila jambo ambalo Mungu amewaamru wao walitende. Msambamba huu waweza kufasiriwa kwaiti kauli moja inayowasilisha matakwa ya kutunza amri zote za Yahweh. : "Yapasa mzitii sheria na namri zote"

Ili kwamba mpate kutembea katika hizo

Kutii amri za Yahweh kumezunguziwa kana kwamba kulikuwa njia ambayo juu yake mtu hutembea. : "ili kwamba mweze kusimamia mwenendo yenu kulingana na hizo.

Leviticus 18:6

wake za baba yako

Wakati mwingine wanaume walikwa na zaidi ya mke mmoja. Mungu hakumruhusu mwana kulala na mwanamke yeyote aliyeolewa na baba yake.

Leviticus 18:9

ama ni binti ya baba yako au ni binti ya mama yako

Hii humaanisha mwanaume hawezi kulala na iwapo wa mazazi wale wale hata kama ana mama au baba tofauti.

ama aliyelelewa nyumbani mwenu au mbali nawe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ama alikulia nyumbani kwenu au mbali"

Usilale na binti ya mke wa baba yako,

Maana mbili zinazowezekana ni 1) "usilale na dada yako wa kambo au 2) "usilale na dada yako wa kunyonya." Hapa mwanaume hana baba au mama mmoja na mwanamke. walikuwa kaka na dada wazazi wao walipooana.

Leviticus 18:12

Usimkaribie kwa kusudi hilo

"Usimwendee kwa kusudi la kulala naye"

Leviticus 18:15

usilale naye

Yahweh analirudiia hili ili kuisisitiza amri hii.

Leviticus 18:17

uovu, ufisadi, upotovu

Ile misemo "uovu" na "ufisadi" yote mawili humaanisha jambo lolote linalopingana na tabia na mapenzi matakatifu ya Mungu.

Neno "uovu" linapoweza kuelezea tabia ya mtu, neno, ufisadi linaweza kuhusiana na tabia tabia ya mtu, Hata hivyo, misemo yote miwili hufanana katika maana.

Ule msemo" upotovu" humaanisha ile hali ya kuwawepo watu wafanyapo mambo maovu.

Yale matokeo ya uovu huonyeshwa wazi katika namna watu wanavyotendea vibaya wengine kwa kuua, kuiba, kulahgai, au kuwa wakatili na kutokuwa na huruma.

MAPENDEKEZO YA UFASIRI Kwa kutegemea namuktatha, ile msemo "ovu" na "fisadi" yaweza kufairiwa "baya" au"-enye dhambi" au "-siyo adilifu."

Njia nyingine za kufasiri haya zaweza kujumuisha, "siyo -ema, "isiyo nyofu" au "isiyo adilifu."

Hakikisha kwamba yale maneno au virai vinavyotumika kufasiri misemo hii ni vyenye kufaa kwenye muktadha vilivyo vya asili katika lugha lengwa.

uhai, ishi, maisha, -wa hai

Tazama maelezo ya sura 18:3

Leviticus 18:19

hedhi

Hiki ni kipindi cha majira ambapo mwanamke anapotokwa damu kutoka kwenye mji wake wa mimba.

yeye ni najisi

Tazama maelzo ya sura ya 13:20

mke wa jirai yako

"muke wa mwanaume yeyote"

Leviticus 18:21

Taarifa kwa ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa watu kisichowapasa kukifanya ambacho kingewachafua wao.

Msiwatoe watoto wenu ili kuwapitisha kwenye moto

Kile kirai "kuwapitisha kwenye moto" humaanisha kuwachoma kitu kwa moto kwa dhabihu. : "Msiwachome moto wato wenu wangali hai"

msije mkalikufuru jina la Mungu wenu

"KNeno "kukufu" hapa ni kufedhehesha. Neno "jina" humwakilisha Mungu mwenyewe. : "msimfedheheshe MUngu wenu."

Leviticus 18:22

hili lingekuwa uovu

"Uovu" hapa hurejelea ukiukaji wa mfumo wa vitu vya asili kama Yahew alivyovitarajia viwe.

Leviticus 18:24

mataifa yamechafuliwa

Hii humaanisha vikundi vya watu vinavyoishi huko Kanaani. Hii inafaa kufasiriwa ili kwamba ule msemo "mataifa" uwekwe wazi kuwa ni "watu." : "watu wa mataifa walijichafua wenyewe"

Nayo nchi imenajisiwa

"Watu waliichafua nchi"

nayo nchi ikawatapika wakazi wake

Yahweh akiwawaondoa watu kwa nguvu kutoka katika kunazungumziwa kana kwamba nchi ilikuwa mtu ambaye aliwatapika watu. : "Ikiwa aliwaondowa watu kwa nguvu kutoka katika nchi, kama vile mtu atapikavyo chakula"

Leviticus 18:26

aina yoyote ya mambo haya ya machukizo

"lolote haya mambo ya kuchukiza"

haya ya machukizo

Hii iinamaanisha "mambo haya ya machukizo."

Kwa hiyo, muwe waangalifu

"Kwa hiyo basi iwenu waangalifu"

ili kwamba nchi isiwatapike nyinyi baada ya kuwa mmeinajisi, kama ilivyowatapika wale watu

Tazama maelezo ya sura 18:24. : "ili kwamba ninawaondoa kwa nguvu mtoke katika nchi...kama nilivyowaondoa kwa nguvu hao watu"

Leviticus 18:29

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anamaziliza kumwambia Musa kinachowapasa watu kunda.

watu...watakatiliwa mbali kutoka miongoni mwa watu wao

Tazama lilifasiwa katrika sura zilizotangulia.

ambazo zilitendwa hapo kabla yenu

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. :"ambayo watu waliyatenda hapa kabla yenu"

kwazo

"Kwazo" hapa hurejelea desturi zenye machukizo

Leviticus 19

Leviticus 19:1

muzishike Sabato zangu

"tunza Sabato zagu" au "heshimu siku yangu ya mapumziko"

Msizigeukie sanamu zisizo na thaman

Kule kuabudu sanamu kumezunguzungumziwa kana kwamba ilikuwa ni kugeukia kwao kimaumbile

Leviticus 19:5

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa kinachowapasa watu kukifanya

utatoa ili kupata kibali.

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. Maana zinazowezekana ni 1) Yahweh atampokea mtu atoaye hiyo dhabihu. : "yapasa uilitoe ili kwamba huenda atakupokea" au 2) Yahweh ataikubali dhabihu kutoka kwa huyo mtu. : "yakupasa kuitoa ili kwamba huenda Yahweh ataipokea dhabihu yako."

sharti iliwe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Sharti muile"

lazima kiteketezwe kwa moto

Tazama maelezo ya 19:6

Endapo kitaliwa hata kidogo

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Ikiwa utakula hata sehemu hata yake yoyote"

Hakitakubalika

Kula sadaka baada ya wakati ulioteuliwa ni kwenda kinyume na Mungu na huongeza hatia ambayo dhambi ilikuwa iifunike. Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "usiikubali hiyo kwa ulaji"

kila akilaye ni lazima atachukua hatia yake

Ile hati ya mtu imezungumziwa kana kwamba illikuwa kitu chenye maumbile ambacho mtu hukibeba. Neno "hatia" hapa huwakilisha ile adhabu kwa hatia hiyo. : Kila mmoja...anawajika kwa hatia yake mwenyewe" au Yahweh atamwadhibu kila mmoja...kutokana na dhambi zake mwenyewe

Mtu huyo sharti atakatiliwa mbali na watu wake

Tazama lilivyofasiriwa katika 7:19 : "inawezekana mtu huyo asiendelee kuishi kuishi miongoni mwa watu wake" au "ni lazima mmtenge mtu huyo na wa watu wake"

Leviticus 19:9

Unapovuna mavuno ya ardhi yako, usivune hata pembezo mwa shamba lako kabisa

"Unapokusanya mazao yako, usiyakusanye yote hata mipakani mwa mashamba yako"

wala hutakusanya mabaki ya mavuno yako yote

Hii hurejelea ile desturi ya kurudia kuvuna shambani kama kipindi cha pili cha kukusanya mazao yaliyobaki baada ya kipindi cha kwanza. Maana kamili ya maelezo haya yaweza kuwekwa wazi. : "na usirudi nyuma uvunapo shambani na kuokota masalio yote uliyoyaachia nyuma"

Leviticus 19:11

Usiape kwa jina langu kwa uongo

"Usilitumia jina lwangu kuapa juu ya jambo fulani ambalo siyo la kweli.

Leviticus 19:13

Usimgandamize jirani yako wala kumwibia

"Jirani" hapa humaanisha "yeyote"Maana ya hili yaweza kuwekwa wazi. : "usimuumize wala kumwibia yeyote"

Usishikilie malipo ya kibarua usiku kucha hata asubuhi

Yahweh anamwamru mwajiri kumlipa kwa haraka mtumshi wake mara kazi yake inapokamilika siku hiyo hiyo. Maana kamili ya tamko hili yaweza kufanywa wazi.

Leviticus 19:15

Usisababishe hukumu ikawa ya uongo

Hii hasi ya maradufu imetumika kusisitiza. Inaweza kuelezwa katika nji chanya. : "Hukumu kwa haki siku zote"

Usionyeshe upendeleo kwa mtu fulani eti kwa kuwa tu yeye ni masikini na usionyeshe upendeleo kwa mtu fulani eti kwa kuwa tu yeye ni mtu muhimu

Yale maneno "masikini" na "muhimu" ni mambo mawili yenye kukithiri, ambayo kwa pamoja humaanisha "yeyote." : "Haikupasi kuonyesha upendeleo kwa yeyote kwa msingi wa kiasi cha wingi wa fedha walizo nazo.

amua juu ya jirani yako kwa haki

""mhukumu kila mmoja kwa kulingana na haki"

Usiende huku na huko ukisema habari za uchochezi

"Usiende huku na huko kwa watu wengine huku ukisengenya"

Leviticus 19:17

Usimchukie ndugu yako moyoni mwako

Kule kumchukia ndugu yako kwa kuendelea kumezungumziwa kana kwamba kulikuwa kumchukia mtu ndani ya moyo. : "Ussimchukie ndugu yako wa kuendelea"

Mkemee jirani yako kwa heshima

"Yapasa umrekebishe anayetenda dhambi"

Leviticus 19:19

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa yawapasayo watu kutenda.

vazi lililofumwa kwa kutumia nyuzi za rangi mbili tofauti zilizochanganywa pamoja

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "vazi ambalo mwingine alilitengeneza kutokana na nyuzi za aina mbili"

Leviticus 19:20

aliyeposwa na mume mwingine

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "liyeahidiwa kuolewa na mwanamume mwingine"

lakini ambaye hajakombolewa au hajaachwa huru

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ambaye mume wake mtarajiwa hajamkomboa au kumpa uhuru"

lazima waadhibiwe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "niyapasa kumwadhibu huyo msichana mtumwa na hyuo mwanaume aliyelala naye"

Hawatauawa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Haiwapasi kuwaua"

mtu huyo alete sadaka yake ya hatia kwenye ingilio la hema la kukutania—kondoo dume iwe sadaka ya hatia

Huyo mwanaume atalazimika kuleta kondoo dume kwenye ingili la hema ya kukutania kuwa sadaka ya hatia kwa Yahweh"

Nayo dhambi iliyotendwa itasamehewa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Naye Yahweh ataisameheme dhambi aliyoitenda"

Leviticus 19:23

Taarifa kwa Ujulma

Yahe anaendelea kumwambia Musa yawapasayo watu kutenda.

kisha mtayahesabu matunda yatakayozaliwa kuwa yamekatazwa kuliwa. Halitaliwa

Yahweh analirudia katazo ili kulikazia na kuweka wazi kwamba ni lazima kwa miaka mitatu ya kwanza ya mti kuzaa matunda. Ni lazima kuwe na kipindi maalum kwa miti kuachwa peke yake. : "nawe hutakula matunda ya miti kwa miaka mitatu ya kwanza"

Tunda litakatazwa kwako

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Nimelikataza tunda kwako"

Nalo alitaliwa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Sharti usilile"

Leviticus 19:26

damu

Msemo "damu" humaanisha kimiminika chekundu kinachotoka kwenye ngozi ya mtu panapokuwa na jeraha au kovu. Damu huleta virutubisho vitoavyo uhai kwa mwili mzima wa mtu.

MAELEZO YA UFASIRI

roho, -a kiroho

Msemo roho hulenga sehemu ya watu isiyo na maumbile isiyoweza kuonekana. Mtu anapokufa, roho yake huuacha mwili wake. Pia "roho" yaweza kumaanisha tabia au hali ya kujisikia.

MAPENDEKEZO YA UFASIRI

uweza, weuzo

Ule msemo "uweza" humaanisha uwezo wa kufanya mambo au kusababisha mambo yatokee, mara kwa mara kwa kutumia nguvu kubwa. "Uwezo" humaanisha watu au roho zenye uwezo wa kusababisha mambo kutokea.

MAPENDEKEZO YA UFASIRI

Leviticus 19:29

Usimwaibishe binti yako kwa kumfanya kahaba, la sivyo taifa litaangukia kwenye ukahaba na nchi itajawa na uovu

Yale maneno "taifa" na "nchi" huwakilisha watu wakaao humo. Watu wengi wanaotenda ukahaba na wale wengine wanaotenda matendo ya uovu wamezungumziwa kana kwamba wameangukia au wamejawa na mambo hayo. : "Watu wataanza kufanya ukahaba na mambo mengi maovu"

Leviticus 19:31

wafu au roho wachafu

Maana zinazowezekana ni 1) wale "waf" ana "roho" ni vitu viwili tofauti 2)kwamba huku ni kujirudiarudia kunakomaanisha "roho za watu waliokufa"

msiwatafute, la sivyo watawanajisi ninyi

"Msiwatafute hao watu. kama mtafanya hivyo, watawachauweni nyinyi"

Leviticus 19:32

Ni lazima usimame

Kusimama mbele za ya mtu mwingine ni ishara ya kuheshimu.

mtu mwenye mv

mtu mwenye mvi- Hii humrejelea mtu ambaye nywele zake zimekuwa nyeupe kutokana na umri, au mtu mzee."

Leviticus 19:33

Mgeni, -a kigeni, mpitaji

Ule msemo "mgeni" humrejelea mtu anayeishi katika taifa lisilo lake mwenyewe. Jina lingine la mgeni ni "mpitaji"

Katika Agano la Kale, musemo huu hasa humlenga yeyote anayetoka katika kikundi cha watu walio tofauti ya watu aliokuwa akiishi miongoni mwao.

Mgeni pia ni mtu ambaye lugha na utamaduni wake ni tofauti na ule wa kwako

Mathalani, Naomi na familia walipohamia Moabu, walikuwa wageni huko. Naomi na binti mkwe wake Ruthu walipohamia baadaye Israeli, Ruthu aliitwa :"mgeni" huko kwa sababu kwa asili hakutokea Israelli.

Mtume Paulo anawaambi Waefeso kwamba kabla hawajamjua Kristo, walikuwa "wageni" kwa Agano la Mungu.

Wakati mwingine "mgeni" hutafriwa kama "mpitaji," lakini, haliwezi kumlenga tu mtu fulani asiyejulikana au asiyefahamika.

Mpende, penda .

Kumpenda mtu mwingine ni kumjali mtu huyo na kufanya mambo yatakayomnufaisha yeye. Kuna maana mbali mbali za "upendo" ambazo baadhi ya lugha zinaweza kuuelza kwa kutumia maneno tofauti: 1. Upendo unaotoka kwa Mungu wenyewe hulenga juu mema kwa ajili ya wengine, hata kama haujinufashi wenyewe. Iana hii ya upendo hujali wengine, haijalishi wanafanya nini. Mungu mwenyewe ni pendo na ndiye asili ya upendo wa kweli.

. Yesu alionyesha aina hii ya upendo kwa kujitoa dhabihu uhai wake ili kutokoa sisi kutoka dhambini na kifoni. Yeye aliwafundisha pia wanafunzi wake kuwapenda wengine kwa kujitoa dhabihu.

. Watu wanapowapenda wengine kwa aina hii ya upendo, huhusisha matendo yanaoonyesha kwamba mtu mwingine anafikiri juu ya kitakachosababisha mtu mwingi kufanikiwa. Upendo wa aina hii hasa huhusisha kuwasamehe wengine.

. Katika toleo la ULB, neno "upendo" humaanisha upendo wa kujito dhabihu, isipokuwa maelezo yanapoashiria kuleta maana nyingine

  1. Neno lingine katika Agano Jipya humaanisha upendo wa ndugu au upendo wa kirafiki au wa mmoja wa wanafamilia.

. Msemo huu hulenga upendo wa kibinadamu baina ya marafiki au ndugu.

. Linaweza kutumiwa pia katika mazingira kama vile, "wanapenda kukaa kwenye viti vya mbele katika karamu." Hii inamaanisha kwamba "wanapenda sana" au wanatamani sana kufanya hivyo.

  1. Neno "upendo" pia laweza kumaanisha mapenzi baina ya mwanaumme na mwanamke. 4. Katika maelezo ya kitamathali , "Yakobo nimempenda, lakini Esau nimemchukia," ule msemo "nimempenda" humaanisha Mungu kumchagua Yakobo kuwa katika uhusiano naye wa kimaagano. Hili pia laweza kufasiriwa kama "aliyechaguliwa." Ingawaje Esau pia alibarikiwa na Mungu, hakupewa upendeleo wa kuwa katika agano. Ule msemo "nimemchukia" hapa umetumka kitamathali kumaanisha "aliyekataliwa" au "asiyechaguliwa."

MAPENDEKEZO YA UFASIRI . Isipokuwa imeashiria vinginevyo kwenye maelezo ya kiufasirineno "upendo katka kwenye toleo la ULB humaanisha aina ya upendo wa kujitoa dhabihu ambao hutoka kwa Mungu

. Baadhi ya lugha zaweza kuwa na neno maalum kwa upendo usio wa kibinafsi waenye kujitoa dhabihu alionao Mungu. Njia za kuufasiri upendo huuzaweza kuwa pamoja na, "ungalizi wa kujitolea kwa uaminifu" au "jali kwa bila uchoyo" au "upendo kutoka kwa Mungu." Hakikisha kwamba neno linalotumika kufasiri upendo wa Mungu linawez kujumuisha kutupilia mbali masilahi ya mtu ili kunufaisha wengine na kupenda watu bila kujali wanachofanya

. Wakati mwingine neno "upendo" la Kiingereza huelezea uangalizi wa ndani walionao watu kwa ajili ya marafiki na wanafamilia. Baadhi ya lugha zingeweza kulifasiri neno au kirai hiki

. Baadhi ya lugha zinaweza kuwa na

Leviticus 19:35

usitumie vipimo vya udanganyifu

Hii hukataza desturi ya utuumiaji wa makusudi wa zana zinzosababisha usomaji usio sahihi wakati wa kupima vitu.

Efa

Hiki kilikuwa kipimo cha nafaka.

hini

Hiki kilikuwa kipimo kwa ajili ya vimiminika

Sharti uyatii...na kuyatenda

Virai hivi humaanisha kitu kile kile na husisitiza amri ya kutii.

Leviticus 20

Leviticus 20:1

atakayemtoa mtoto wake yeyote kwa Moleki

Wale waliomwabudu Moleki waliwatoa dhabihu watoto wao kwake kwa njia ya moto. Maana kamili yaweza kuwekwa wazi. : "auaye watoto wake kama sadaka kwa Moleki"

hakika atauawa. Ni lazima watu wa nchi wamponde kwa maw

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Watu katika nchi watamponda kwa mawe mpaka kufa

Leviticus 20:3

Pia nitaukaza uso wangu dhidi ya mtu huyo

KIle kirai "kaza uso wangu dhidi" ni nahau inayomaanisha "kumkata." : "Pia Nitamkataa" au "kumpinga vikali'

amemtoa mtoto wake

"amemtoa dhabihu mtoto wake"

ili kupatia unajisi mahali pangu patakatifu na kulinajisi jina langu takatifu

"na kwa kufanya hivyo, ampachafua mahali pangu patakatifu na kulinajisi jina langu takatifu.

najisi jina langu takatifu

Jina la Mungu humwakilisha Mungu na heshima yake. : "dunisha heshima yangu" au "kiunivunjia heshima mimi"

watayafumba macho yao kwa

Kile kirai "kufumba macho yao" huashiria "hawawezi kuona" na huwakilisha kutokuwa na uwezo wa kuelewa kwao. : "kutojali" au "puuzia"

ajifanyaye kahaba ili kufanya umalaya na Molek

Kirai hiki huwafananisha na kahaba wale wasiokuwa waaminifu kwa Yahweh. ; "yeye asiyekuwa mwaminifu kwa Yahweh"

Leviticus 20:6

ili kufanya ukahaba na

Kirai hiki huwalinganisha na kahaba wale watu wasiowaaminifu. : "kwa kufanya hivyo, wanatafuta ushauri kwa roho badala ya kuutafuta kwangu

kaza uso wangu dhidi

Tazama maelezo ya sura20:3

Leviticus 20:8

Maelezo kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa yawapasayao watu kutenda.

Mtazitunza amari zangu na kuzifuta

Yale maneno "tunza" na "fuata" kimsingi humaanisha kitu kimoja. Yametumika pamoja ili kusisitiza kwamba ni lazima watu wamtii Mungu.

hakika mtu huyo atauawa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. :"Yapasa kuua hakika"

Leviticus 20:10

Mwanaume yeyote afanyaye uzinzi na mke wa mwanaume mwingine, yaani, yeyote anayezini na mke wa jirani yake

Maana kamili sentensi hii yaweza kuwekwa wazi. : "Yule mwanaume aziniye na mke wa mtu mwingi"

lazima wote wawili wauawe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "sharti mtawaua wote wawili"

anayelala na mke wa baba yake ili kukutana naye kimwili

Hii ni ni njia ya upole ya kusema kwamba anafanya ngono na mke wa baba yake. Kuna baadhi ya lugha hutumi virai vya moja kwa moja kama vile "kufanya ngono na mke wa baba yake."

Wametenda upotovu

Hapa Mungu anamwita mwanawume anayelala na mke wa mwanae "potovu" , kuw ni dhambi mbaya sana. Tanzama katika sura 18:22 lilivyotafasiriwa ne "uovu"

Leviticus 20:13

mwanaume analala na

Tazama ililivyofasiriwa katika 20:11-12

kama alalavyo na mwanamke

Namana anavyomtendea mwanaume ndivyo angemtendea mwanamke. : "ni kama vile tu angelifanya na mwamke"

jambo lililo ovu.

"jambo la aibu" au "jambo la kuchukiza"

Hakika watauawa

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yawapasa kuwaua hakika"

mwanaume huyo na manamke huyo

Tazama maelezo ya sura 20:12

Leviticus 20:15

hakika atauawa

Tazama maelezo ya sura 20:12

ni lazima mmuuwe mwanamke huyo pamoja na mnyama. Kwa hakika ni lazima wauawe

VIshazi vyote viwili humaanisha kitu kimoja. Vina sisitiza kwamba mwanamke an mnyama sharti wauawe.

Kwa hakika ni lazima wauawe

Tazama maelezoya sura 20:12

Leviticus 20:17

mwanaume analala na

Tazama maelezo hapo juu

ama ni binti ya baba yake au binti ya mama yake

Tazama katika sura zilizotangulia

Ni lazima wakatiliwe mbali watoke

Tazama maelezo ya sura 7:19

Ni lazima aibebe hatia yake

Kirai hiki humaanisha kwamba mtu anawajibika kwa thambi yale. : "Yeye anawajibika kwa dhambi yake" au "Ywawapasa kumwadhibu yeye"

kipindi cha hedhi

wakati ambapo mwanamke anatokwa damu kutoka katika tumbo lake la uzazi

atakuwa amefunua mtiririko wa damu yake, chanzo cha damu yake.

Kirai hiki kinafananisha kule kufanya ngono na mwanamke wakati akiwa kwenye kipindi chake hedhi kuwa ni sawasawa na kufunua kitu mambacho kilipaswa kubakia kimefichwa. Ule uhalisia kwamba hili liliikuwa ni jambo la aibu kukifanya linaweza kuwekwa wazi. : "amefanya jambo la aibu kwa kufunua kmtirirrko wake wa damu"

Ni lizima wote wawili wakatiliwe mbali

Yaweza kuwekwa wazi kwanini hili yapasa litendeke. : "kwa sababu wamefanya jambo hili la aibu, ni lazima wote wawili, mwanaume na mwanamke wakatiliwe mbali"

Leviticus 20:19

alalaye na

Tazama lilivyofasiriwa hapo juu

Ni lazima utabeba hatia yako mwenyewe

Tazama lilivyofasiriwa hapo juu

nitaondolea mbali mali yoyote amabayo watoto wao wangerithi kutoka kwa wazazi wao

Matleo mengi ya Biblia hulifasiri hili kama "watakufa bila kuzaa watoto."

Leviticus 20:22

ile nchi ambayo ninawaleta kuishi isiwatapike nyinyi

Tazama maelezo ya sura ya 18:24

Msienende katika

Kufanya matendo ya waabudu sanamu kumezungumziwa kana kwama ni kutembea katika njia zao. : "haiwapsi kufuata"

nitayafukuza

"ondoa"

Leviticus 20:24

nchi itiririkayo amaziwa na asal

Kile kirai itirirkayo maziwa na asali" humaanisha "iliyotajiri na yenye mazo yenye chakula cha kutosha kwa kila mmoja." : "nchi iliyonzuri kwa mifugo na kilimo" au "nchi yenye mazao"

Leviticus 20:26

nimewatenga nyinyi

"Nimewatofautisha nynyi" au "Nimewaweka kando"

Leviticus 20:27

anayeongea

Ajaribuye kuwasiliana na"

hakika atauawa

Angalia maelezo yaliyotolewa kwenye misitari mingine kwanye sura zilizotanguli.

Leviticus 21

Leviticus 21:1

Jitia unajisi mweneyewe

Tazama maelezo ta sura 13:20

miongoni mwa watu wake

"miongoni mwa Waisraeli"

bikira

Hii yaweza pia kufasiriwa mwanamke kijana"

Leviticus 21:4

pembe

"ncha"au "sehemu yoyote"

Watakuwa watakatifu

"sharti watengwe"

hawataliaibisha jina la Mungu wao

Neno "jina" limetumika kuwakilisha tabia ya Yahweh. : "wasije wakalitia aibu heshima ya Mungu" au wasije wakamfedhehesha Mungu wao"

Leviticus 21:7

Hawataoa

"Makuhani hawataoa"

kwa sababu wametengwa

"kwa sababu wamewekwa kando" (UDB)

Utamtenga

"nyinyi watu itawapasa kuwatendea makuhani kama watakatifu"

kwa sababu yeye ndiye anayetoa mkate kwa Mungu wako

"Mkate" huwakilisha chakula kwa ujumla. Yahweh huwa hali hasa matoleo haya. Yahweh huwa hali chakula isipokuwa wakuhani ndiyo walikula chakula hicho.

Ni lazima ateketezwe kwa moto

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Ni sharti mmcho moto hata kufa"

Leviticus 21:10

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia kile ambachi makuhani kinachowapasa kufanya.

Mafuta ya upako

Hii ni kumbukumbu kwa mafuta ya upako yaliyotumika kwenye ibada ya ya kumweka wakfu kuhani mkuu mpya. Maana kamili ya tamko hili yaweza kufanywa wazi.

ambaye mafuta ya upako yamekwisha kumiminwa kichwani pake, na ambaye amekwisha kuwekwa wakfu

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "amabye juu ya kichwa chake walimimina mafuta ya upako na kumweka wakfu"

kamwe hataziacha wazi nywele zake wala hatazirarua nguo zake

Kuacha nywele wazi na kurarua nguo zilikuwa ni ishara ya kuomboleza. Maana kamili ya tamko hili yaweza kufanywa wazi.

hataondoka eneo takatifu la hema la kukutania

Hii haminishi kwamba kuhani mkuu asingeweza kuondoka . Mungu hakumruhusukuondoka ili kuzunka kwa ajili ya mtu mwingine aliyekufa'

Leviticus 21:13

kutoka mipoongoni mwa watu wake

"kutoka miopngoni mwa kabila lake mwenyewe, kabila la Lawi"

asiwatia unajisi watoto wake miongoni mwa watu wake

Kwa kuoa mwanake asiyemtkatifu au asiye na hofu ya Mungu, kuhani angeweza kuwa na watoto wasiofaa kuwa makuhani. : "ili kwamba asiwe na watoto wasiostahili kwa njia ya kuoa mwanamke asiyemcha Mungu.

Leviticus 21:16

asisogee kutoa chakula kwa Mungu wake

Ile maana kamili ya kauli huii inaweza kufanywa wazi. : "impasi kuja mbele ili kuteketeza sadaka ya kuteketeswa ya chakula cha Mungu juu ya madhabahu.

Leviticus 21:18

asimkaribie Yahweh

Ilipasa kuhani awe na viwango maalum vya kimaumbile ili kumkaribia Yahweh. Hii haimaanishi kwamba kasoro za kimaumbile yalikuwa ni matokeo ya kutokuwa mwadilifu au kwamba watu alio na kasoro za kimaumbile hawana uwezo wa kumkaribia Yahweh.

aliyeharibiwa uso au kupungukiwa na viungo mwilini,

"ambaye mwili au uso wake umeharibiwa"

kutoa mkate wa Mungu wake

"Mkate" hapa huwakilisha chakula kwa ujumla. : "kufanya matoleo ya chakula juu ya madhabahu ya Mungu"

Leviticus 21:22

Anaweza

"Anayeweza" hapa ni yule kuhani aliye na kasoro za kimwili.

Kula chakula cha Mungu wake

"kula matoleo ya chakula ya Mungu wake." sehemu ya dhabihu ilikuwa ya makuhani na ingeweza kuliwa.

Wanawe

"Wana wa Aroni"

Leviticus 22

Leviticus 22:1

waambie wajiepushe na vitu vitakatifu

"waambie wakati wanaotakiwa kujiepusha na vitu vitakatifu." Yahweh anataka kuelezea mazingira ambayo kuhani huwa najisi na haruhusiwi kugusa vitu vitakatifu.

katika vizazi vyenu

"tangu sasa na kuendelea"

wakati akiwa najisi

Tazama maelezo ya sura 13:20

sharti mtu huyo akatiliwe mbali atoke mbele zangu

Yule kuhani asiyeweza tena kumtumika Yahweh amezungumziwa kana kwamba mtu huyo amekatwa kutoka mbele za Yahweh, kama mtu angekata kipande cha nguo au tawi mti kutoka kwenye mti. Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. "Mtu huyo hataweza kamwe kutumika kama kuhani"

Leviticus 22:4

ungonjwa wa ngozi wa kuambukiza

ugonjwa ujuu ya ngozi unaosambaa kwa urahisi kutoka mtu mmoja kwenda kwa mwingine

kutoka mwilini mwake

Tazama maellezo ya sura 15:1

mpaka atakapotakasika

Tama maelezo ya sura ya 13:23

yeyote agusaye kitu chochote kilichonajisi

Tazama maelzo ya sura ya 13:20"

wa njia ya kugusa maiti,

"kwa kugusa mwili wa mfu"

dhabihu iliyofanywa kwa Yahweh

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wautendaji. : "dhabihu ambayo mtu mwingine ameitoa kwa Yahweh"

au yeyote agusaye mnyama atambaaye atakayemtia yeye unajisi, au mtu yeyote atakayemfanya nyeye kuwa ajisi

Hii yaeza kfanywa wazi. : "au yeyote aliyenajisi kutokana na kugusa manyama ataambaye au kutokana na kugusa mtu aliyenajisi"

yeyote agusaye kitu chochote kisichosafi atakuwa najisi

Hii yaweza kufanywa wazi. : "au yeyote aliyenajisi kutokana na kugusa mnyama aliye mlemavu au kutokana na kugusa mtu aliye najisi"

hata jioni

"mpaka machweo"

kuhani ... atakuwa najisi

Tazama maezo ya sura ya 13:23

Leviticus 22:7

ndipo atakuwa safi

Tazama maelezo ya sura 13:23

uliookotwa au mnyama aliyeraruliwa na wanyama pori

Hii aweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ambaye mtu mwingine amemwokota akiwa amekufa au yule ambaye mnyama pori kamrarua"

Leviticus 22:10

Maelezo kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa yawapasyo Aroni na wanawe kutenda.

Leviticus 22:12

mchango wa matoleo matakatifu

Neno "mchango" laweza kufasiriwa kirai che kitenzi. : "matole matakatifu ambayo watu wamechangia"

Leviticus 22:14

naye atamlipa kuahani kwa ajili ya hicho; itampasa kuongeza moja ya tano juu yake

moja ya tano juu yake- maana zinazowe kuwa ni 1) kwamba mtu alipaswa kureje chakula kilicholiwa pamoja na chakula cha aina ile ile au 2) kwamba mtu huyo alipwa kulipa fedha kwa kuhani kawa jili ya chakula alikila yeye.

moja ya tano juu ya tano

moja ya tano juu yake- Hii ni sehemu moja kutoka kwenye sehemu matano zilizosawa.

kutoheshimu vitu vitakatifu

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yawapasa kukuvitendea kwa heshima hivyo vitu vitakatifu"

ambavyo vimeinuliwa juu na kuletwa

Kile kirai "vimeinuwa juu" hurejelea ile ishara ya heshima ninayowakilisha utoaji wa kitu fulani kwa Yahweh. Kimsingi humaanisha kitu kile kile kama "kilichotolewa." : "kile walichokitoa"

wakajisababishia wenyewe kuchukua dhambi amabyo ingewafanya kuwa na hatia

Dhambi imezungumziwa kana kwamba kilikuwa chombo ambacho watu wanaweza kukibeba. Maana za weza kuwa 1)Wangeweza kuwajibika kwa dhambi na kuwa na hatia. : "Wangekuwa na hatia kwa ajili ya dhambi waliyoitenda" au 2)neno "dhambi" kibadala cha cha adhabu kwa ajili ya dhambi waliyoitenda. : "Wangepokea adhabu kwa sababu ni wenye hatia"

Leviticus 22:17

mgeni

"mpitaji"

ikubalike,

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa kiutendaji.: "iwapo Yahweh ataikubali" au "iwapo, Mimi, Yahweh, nitaikubali"

Leviticus 22:20

ili ikubalike

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "kwa Mimi kuikubali" au "kwa Yahweh kuikubali"

Leviticus 22:22

waliojeruhiwa, wala waliotiwa kilema

Maneno haya humaanisha kasoro zilizosababishwa na ajali.

wenye upele, vidonda vitokavyo usaha, wala wenye vigaga

Haya humaanisha aina za magonjwa ya ngozi.

haitapokelewa.

"Yahweh ataikubali"

mlemavu au aliyedumaa

Maneno haya yanamaanisha kasoro ambazo mnyama anazo tangu kuzaliwa

Leviticus 22:24

Usilete mkate wa Mungu wako

"Kate" hapa huwakilisha chakula kwa ujumla. Mungu hakula dhabihu hasa. Makuhani wangetoa dhabihu juu ya madhabahu ya Mungu, na wangekula sehemu ya nyama. : "hataleta mnyama kuwa matoleo ya chakula kwa Mungu wenu"

Kutoka mkononi mwa mgeni

Neno "mkono" huwakilisha mtu mzima. Inaonyeshwa kwamba Waisraeli wasingeweza kutumia wanyama kama dhabihu iwapo wangewanunua kutokwa wageni ambao walihasi wanyama wao wakifanya wasikubalikekwa Mungu. : "ambaye mgeni amewapa , kwa sababu wao huhasi wanyamaa wao"

hawatapokelewa kabisa kwa ajili yako

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "Yahweh hatawapokea kutoka kwenu"

Leviticus 22:26

anaweza kupokelewa

"unaweza kuikubali"

iliyofanywa kwa moto

"kwa ajili ya sadaka ya kuteketeza"

Leviticus 22:28

Ni lazima iliwe

"Ni lazima uile"

iyo hiyo inayotolewa

"uliyoitoa dhabiihu"

Leviticus 22:31

kuzishika amri zangu na kuzifuata

Yale maneno "Shika"na "fuata" humaanisha kitu kilekile. Nayo husisitiza kwamba ni lazima watu watii ammri za Mungu, : "tii amri zangu"

2Msiliabishe jina langu takatifu

Neno "jina" hapa humwakilisha Yahweh mwenyewe na sifa zake njema. : "msiniabishes mimi Au "msiiabishe sifa yangu njema"

Ni lazima nitambuliwe kuwa ni mtakatifu na watu wa Israeli

: "Watu wa Israeli wanitambue kwamba mimi ni mtakattifu"

Leviticus 23

Leviticus 23:1

sikukuu zilizoamriwa kwa ajili ya Yahweh

Hizi ndizo zilikuwa sikuu ambazo Bwana aliamru majira yake. Watu walikuwa wamwabudu yeye kwenye sikukuu hizi. : "Sikukuunkwa ajili ya Yahweh" au sikukuu za Yahweh"

Leviticus 23:3

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa yawapayo watu kutenda katika nyakati za ssiku maalum.

siku ya saba ni Sabato ya kupumzika kabisa

hili ni jambo ambalo watu yawapasa kulifanya kuwa mazoea yao. Kila baada ya siku sita katika watakazofaanya kazi, nilazima wapumzike katika siku ya saba.

kusaniko takatifu

Yale makwa ambayo watu walikusanyika kumwabudu Mungu katika siku hiyo yamezungumziwa kana kwamba siku hiyo ilikuwa ni kusanyiko. : "siku taktifu, ambayo yawapasa kukusanyika kuniabudu mimi"

Leviticus 23:4

nyakati zilioamriwa

"katika nyakati zake mwafaka"

mwenzi wa kwanza, siku ya kumi na nne ya mwezi ... Siku ya kumi na tano ya mwezi ule ule

Mwezi wa kwanza katika kalenda ya Kiebrania huitia alama siku Yahweh alipowatoa Wasraeli katika nchi ya Misri. siku ya kumi na nne na ya kumi na tano ziko kariru na mwanzo wa mwezi wa Aprili katika kalenda ya Magharibi.

kwenye machweo.

"wakati wa jua kuzama"

Leviticus 23:7

Siku ya kwanza ni lazima mjitenge kwa pamoja

"Yawapasa kuitenga siku ya kwa kwanza ili kukusanyika pamoja" au "Ni lazima muione siku ya kwanza kuwa tofauti na kukusanyika pamoja.

mtamletea Yahweh matoleo ya chakula

Wataiwasilisha kwa Yahweh kwa kuteketeza juu ya madhabahu.

Siku ya saba ni ya kusanyiko takatifu lililotengwa kwa ajili ya Yahweh

Yale matakwa ambayo watu wanayakusanyikia katika siku hiyo yamezungumziwa kana kwamba siku hiyo ilikuwa kusanyiko. Kuwa umetengwa kwa Yahweh humaanisha kwamba wanapokusanyika, ni lazima wamwabudu Yahweh. : "Siku ya saba ni ambayo yawapasa kukusanyika pamoja ili kumwabudu Yahweh.

Leviticus 23:9

mganda wa nafaka wa matunda yake ya kwanza

"mganda wa kwanza" au "kitita cha kwanza cha nafaka."mganda" ni fungu moja la nafaka ambalo mtu amelifunga pamoja.

kwa kuwa litakubalika

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "kwa ajili yaaa kupokelewa na Yahweh" au "Nami nitalipokea"

Leviticus 23:12

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa yawapasayo watu kutenda.

sehemu mbili za kumi ya efa

Efa moja ni sawasawa na lita 22. "lita nne na nusu"

Moja ya nne ya hini

Hini moja ni sawasawa na lita 3.7. : "lita moja"

wala nafaka iliyokaangwa au nafaka mpya

wala nafaka iliyopikwa au isiyopikwa

Hii itakuwa amri ya kudumu katika vizazi vyote vya watu wenu

Tazama lilivyofafanuliwa katika 3:15

Leviticus 23:15

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa yawapasayo watu kutenda.

siku hamsini

"siku 50"

ya saba

Hii ni ya kwaida kwa namba saba

Leviticus 23:17

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumbia Musa yawapasayo watu kutenda

iliyotengenezwa kutokana na mbili ya kumi ya efa. Ni lazima ifanywe kwa unga laini na uliochanganywa na hamira

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. ; "uliyoitengenza kutokana na mbili ya kumi ya efa ya unga na ulioumliwa kwa hamira"

mbili ya kumi ya efa.

Takribani lita 4.5. : "lita nne na nusu"

na kutoa harufu nzuri ya kupendeza kwa Yahweh

Furaha ya Mungu kwa manukato huwakilisha fura furaha yake kwa watu wanaoteketeza matoleo hayo. : "naye Yahweh atapendezwa nanyi" au "impendezayo Yahweh"

Leviticus 23:22

Mtakapovuna mazao ya nchi yenu, Msivune kabisa kabisa pembeni mwa mashamba yenu

"Mkusanyapo mazao yenu, msiyakusanye yote hata kufika mipakani mwa mashamba yenu"

Leviticus 23:23

Katika mwezi wa saba., siku ya kwanza ya mwezi huo

Huu ni mwezi wa saba wa kalenda ya Kiebrani. Siku ya kwanza ni karibu na katikati ya mwezi wa Septemba kwenye kalenda ya Magharibi.

pumzika makini

kipindi cha wakati ambacho kilikuwa cha ibada na siyo kwa ajili ya kazi.

lazima mtoe dhabihu inayofanywa kwa moto kwa Yahweh

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "yawapasa kutoa dhabihu mnayoifanya kwa mto kwa Yahweh" au "ni sharti mteketeze sadaka kwa Yahweh juu ya madhabahu"

Leviticus 23:26

siku ya kumi ya mwezi huu wa saba

Huu ni mwezi wa saba wa kalenda ya Ebrania. Siku ya kumi ni karibu na mwisho wa mwezi wa Septemba katika kalenda ya Magharibi.

siku ya upatanisho

Katika siku hii kila mwaka kuhani mkuu alifanya dhabihu kwa Yahweh ili kwamba Yahweh angeweza kusamehe dhambi zote za watu wa Israeli. : "siku ya dhabihu kwa ajili ya msamaha"

Leviticus 23:28

Maelezo Unganishi

Yahweh anaedelea kumwambia Musa yawapasayo watu kufanya kila mwaka.

azima akatiliwe mbali na watu wake

Tazama maelezo ya sura ya 7:19

Leviticus 23:30

Maelezo ya Kuunganisha

Yahweh anaendelea kumwambia mMusa yawapasayowatun kutenda.

katika siku hiyo

"katika siku ya upatanisho"

Hii itakuwa amri ya kudumu katika vizazi vyote vya watu wenu

Tazama katika sura ya 3:15

Sabato ya pumziko makini

Hii haikuwa Sabato ile ambayo waliishika kila juma katika siku ya saba. Hii ilikuwa ni sabato maalum katika siku ya upatanisho.

yapasa mjinyenyekeze

katika jambo hili, kujinyeyekeza wenyewe kulimaanisha kwamba wasingeku

siku ya tisa ya mwezi

hii humaanisha mwezi wa saba katika kalenda ya Kiebrania. Siku ya tisa ni karibu na mwishoni mwa mwezi wa Septemba katika kalenda ya Magharibi. Hii yaweza kufanywa wazi. : "siku ya tisa ya mwezi wa saba"

Tangu jioni hata jioni

"Tangu machweo mpaka machweo kwenye siku inayofuata"

Leviticus 23:33

siku ya kumi natano ya mwezi wa saba

Hii ni karibu na mwanzoni mwa mwezi wa Oktoba katka lenda ya Magharibu.

Sikukuu ya Vibanda

Hii ni sherehe wakati ambao watu wa Israeli waliishi katika vibanda vya muda kwa siku saba kama njia ya kukumbuka muda walioutumia wakiishi kwenye jangwani baada ya kutoka Misri.

Leviticus 23:37

Hizi ndizo sikukuu zilizoamriwa

Sikukuu hizi zimetajwa katika 23:1-36

Leviticus 23:39

Kuhusu Sikukuu ya vibanda

Tazama katika sura ya 23:33

siku ya kumi natano ya mwezi

Huu ni mwaka wa saba wa kalenda ya Kiebrania. Siku ya kumi na tano ni karibu na mwanzoni na mwezi wa Oktoba kwenye kalenda Magharibi.

mmeyakusanya ndani matunda

"baada ya kuwa mmeyakusanya mazao"

Leviticus 23:40

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea na maelekezo yake juu ya sikukuu ya vibanda.

makuti ya mtende ... matawi ya mierebi kutoka chemchemi za maji

Matumizi ya matawi yanayoweza kuwa ni 1) kujenga vibanda vya muda au 2) kuyapunga kama sehemu ya kusherehekea kwa kwa shangwe, Baadhi ya tafsiri hutamkwa wazi matumizi yake; matoleomengine huacha kuesema uwazi wake.

Mierebi

Miti yenye majani marefu, membamba, ambayo huota karibu na maji.

Leviticus 23:42

wazao wenu, kizazi baada ya kizazi, waweze kujifunza

"kizazi baada ya kizazi" ni nahau inayomaanisha kwa kila kizazi kinachoishi baada ya kingine. "wazao wenu wa kizazi kijacho wwaweze kujifunza" au "wazao wenu wote waweze kujifunza daima"

Leviticus 24

Leviticus 24:1

Taarifa kwa Ujumla

Mungu anampa Musa maelekezo kuhusu vitu vya hekaluni

mafuta halisi yaliyokamliwa kutokana na mizeituni

"mafuta halisi ya zeituni

taa

Hii humaanisha ile taa au zile taa kwenye hema takatifu la Yahweh. hili laweza kufasiriwa kwa uwazi. : "ile taa katika hema la kukutania

Leviticus 24:3

Kauli Unganishi

Mungu anaendelea kumpa Musa maelekezo juu ya vitu katika hema la kukutania

Nje ya pazia lililoko mbele ya sanduku la maamzi

Kile kirai "sanduku la maamzi" huwakilisha ama zile mbao ziliandikwa juu yake au lile sanduka ambalo hizo mbao ziliwekwa ndani yake. Hivi vilitunzwa vema humo mahali patakatifu pa patakatifu, am bacho kilikuwa ni chumba nyma ya pazia ndani ya hema la kukutania. : "Nje ya pazia lililoko mbele ya mbao za sanduku la maamzi" au "Nje ya pazia

pazia

Hiki kilikuwa ni kitambaa kinene kilichoning;inizwa kama ukuta . hakikuwa kama pazia la dirishani la kitambaa chepesi.

tangu asubuhi hata jioni

tangu mawio mpaka machweo" au "usiku mzima"

Hii itakuwa amri ya kudumu katika vizazi vyote vya watu wenu

Tazama maelezo ya sura 3:15

Leviticus 24:5

Maelezo Ungajishi

Mungu anaendea kumwelekeza Musa juu ya vitu kwenye hema la kukutania

mbili za kumi za efa

Hizi ni kama lita 4.5. : "lita nne na nusu"

meza ya dhahabu safi mbele za Yahweh

Meza hii ilikuwa mahali pa takatifu, ambayo ilikuwa kabla ya patakatifu pa patakatifu.

Leviticus 24:7

Maelezo Ungajishi

Mungu anaendea kumwelekeza Musa juu ya vitu kwenye hema la kukutania

Mtaweka uvumba safi kando ya kila safu

Uvumba labda ulifuata baada ya mikate. : "yapasa muweke uvumba safi katika kila safu"

kuwa sadaka ya kuwakilish

Kile uvumba uliwakilishwa cha weza kutamkwa kwa uwazi> "ili kuwakilisha mikate kama sadaka" au kuwa sadak iwakilishayo mikate"

kwa kuwa ni sehemu ya matoleo

"kwa kuwa waliichukua kutoka kwenye matoleo"

matoleo kwa Yahweh yaliyofanywa kwa moto

"sadaka ya kuteketezwa kwa Yahweh" au "sadaka mnayoichoma kwa ajili ya Yahweh"

Leviticus 24:10

Sasa ilitokea

Kirai hiki kianunda sehemu mpya ya kitabu.

akalikufuru jina la Yahweh na kumlaani Mungu

Vilai vyote viwili kimsingi humaanisha kitu kimoja. "akamfufuru Yahweh kwa kumalaani" au alisema mambo maovu kumhusu Yahweh"

Shelomithi

Hili ni jina la mwanamke.

Dibri

Hili ni jina la mwaume.

Leviticus 24:13

Wale wote waliomskia wataweka mikono yao juu ya kichwa chake

Walikuwa waweke mikono yao juu ya kichwa chake kuonyesha kwamba alikuwa mwenye hatia.

Leviticus 24:15

Maelezo Unganishi

Mungu anaendelea kumwambia Musa walichopaswa kumtendea mtu aliyemkufuru Mungu

imempasa kubeba hatia yake mwenyewe

Kuteseka kwa ajili ya dhambi kumezungumziwa kana kwamba alikuwa mtu abebaye hatia yake. : "Sherti ateseke kwa ajili ya dhambi zake" au "ni lazima aadhibiwe"

lazima auawe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. : "ni sharti watu watamuua" au "hakika yawapasa watu kumuua"

Leviticus 24:17

Maelezo Unganishi

Mungu anaendelea kumwambia Musa yawasayo watu kutenda mtu mwingine anapofanya mambo mabaya

ni lazima kwa hakika auewe

Hii yaweza kufasiriwa katika mtindo wa utendaji. "hakika yawapasa kumuua yeyote anayemuua mtu mwingine"

sharti amfidie

Jinsi anavyomfidia kwa weza kutamkwa wazi. : "yapasa amfidie kwa kumpa mwenye mali mnyama aliyehai"

uhai kwa uhai

Hii ni nahau inayomaanisha uhai mmoja ungechukua nafasi ya uhai mwingine. : "uhai mmoja kuchukua nafasi ya uhai mwingine" au "kumfidia yule aliyemuua"

Leviticus 24:19

Maelezo Unganishi

Mungu anaendelea kumwambia Musa yawasayo watu kutenda mtu mwingine anapofanya mambo mabaya

lazima atendewe vivyo hivyo

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "sharti mtende hivyo kwake"

Mvunjiko kwa mvunjiko

Virai hivi vinasisitiza kwamba mtu anapaswa kupokea madhara yale yalele ambayo yeye aliyafanya kwa mwingine.

jicho kwa jicho, jino kwa jin

Tazama aelezo ya sura 24:20

Jino kwa jino

Hii humaanisha jino lililong'olewa kutoka kinywani. : "kama anang'oa jino la mtu mwingine, mojawapo la meno yake litang'olewa" au iwapo anang'oa jino la mtu mwingine, nao watang'oa mojawapo ya meno yake"

Yera kwa jeraha

Hii humaanisha mifupa yenyekuvunjika. : Mfupa uliovunjika kaw amfupa uliovunkia" au "kamaanavunja mfupa wa , mmojawapo wa mifupa yake lazima uvunjwe " au "kama anavunja mfupa wa mtu mwingine, nao watavunja mmojawapo wa mifupa yake"

yeyote auaye mtu lazima auawe

Hii yaweza kutamkwa katika mtingo wa utendaji. : "nao sharti wamuue yeyote auaye mtu"

Leviticus 24:22

wakaitekeleza amri

"wakaitii amri"

Leviticus 25

Leviticus 25:1

hiyo nchi lazima ifanywe iwe ya kuishika Sabato kwa ajili ya Yahweh

Nchi inazunguziwa kana kwamba ilikuwa mtu ambaye angeweza kuitii sabato kwa kupumzika. Ni kama vile tu watu wanavyopaswa kupumzika kila siku ya saba, watu walikuwa waheshimu Mungu kwa kutoilima ardhi katika kila mwaka wa saba.: "yawapasa kuitii sheria ya Sabato kwa kuiacha ardhi ipumzike kila mwaka wa saba kwa ajili ya Yahweh" au "yawapasa uitii Sabato ya Yahweh kwa kutoilima ardhi kila mwaka wa saba"

Leviticus 25:3

mtaikatia matawi mizabibu yenu

Kuikatia matawi mizabibu ni kuyawezesha matunda kukua vizuri.

Sabato ya pumziko la utulivu kwa nchi itashikwa

Kutoilima ardhi nikumezungumziwa kana kwamba ni pumziko la nchi. Hii yawweza kukutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "yawapasa kuishika Sabato ya pumziko makini kwa ajili ya nchi" au "yakupasa kuitii sheria ya Sabato kwa kutoilima ardhi kila mwaka wa saba"

Leviticus 25:5

Hamtasimamia ... wanaoishi pamoja nawe mnaweza kujikusanyia chakula

Katika a 25:5-6 Yahweh anamaanisha hatamruhusu mmiliki wa shamba kuwasimamia wafanya kazi wake na kuivuna nchi kama afanyav miaka mingine sita. Hata hivyo, Yahweh atawaruhusu mtu mmoja mmoja kwenda shambani ili kuokota na kula mda wapatayo.

mizabibu yenu isiyokatiwa matawi

Hii humaanisha kwamba hayupo aliye angaliamizabibu na kukatia matawi kama wafanyavyo katika miaka sita mingine. Hii yaweza kutamkwa atika mtindo wa utendaji. : "mizabibu yenu msiyoikatia matawi"

Chochote ardhi isiyofanyiwa kazi itakachotoa

Chochote kipukacho juu ya ardhi isiyofanyiwa kazi"

ardhi isiyofanyiwa kazi

Hii humaanisha kwamba hakuna mtu aliyeziangalia bustani au mashamba kama wafanyavyo katika miaka sita mingine. Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "bustani zenu msizozitunza"

Chochote ardhi ... itakachotoa

"chochote kiotacho juu ya ardhi"

Leviticus 25:8

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa kiwapassacho watu kutenda.

kutakuwa na Sabato za miaka saba.

"kutakuwa na seti ya miaka saba"

miaka arobaini na tisa

miaka tisa - "miaka 49"

kumi ya mwezi wa saba

Huu ni mwezi wa saba wa kalenda ya Kiebrania. Siku ya kumi ni karibu na mwaisho mwezi wa Septemba katka kalenda ya Magharibi.

Siku ya Upatanisho

Tazama lilivyofasiriwa katia sura ya 23:26

Leviticus 25:10

mwaka wa hamsini

Hii ni namba ya mpango. : "mwaka wa 50"

Yubile kwa ajili yenu

Yubile ulikuwa mwaka ambao Wayahudi walipaswa kurejesha ardhi kwa wamiliki wake wa asili na kuwaacha huru watumwa. : "mwaka wa urejesho kwa ajili yenu" au "mwaka kwenu wa kurudisha ardhi na kuacha huru watumwa"

mali na watumwa ni lazima warejeshwe

Hii yweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "yawapasa kurudisha mali na watumwa"

Leviticus 25:11

Yubile kwenu

Tazama maelezo ya sura 25:10. Nayo yaweza kutamkwa wazi kwa waliyekuwa wakiirejesha hiyo ardhi. : "mwaka ambao mnapaswa kuirejesha ardhi kwangu"

Nanyi mtakula mazao yanayokua yenyewe kutoka mashambani

azama maelezo katika 25:5-7

Leviticus 25:13

mwaka huu wa Yubile

"mwaka huu wa urejesho" au "mwaka huu kurudisha ardhi na kuweka huru watumwa|"

Leviticus 25:15

Taarifa kwa Ujumla

MUngu anaendelea kumwambia Musa yawapasayo watu kutenda.

ambayo yaweza kuvunwa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "nayowea kuyavuna"

Yubile nyingine

"mwaka mwingine wa urejesho" au "mwakamwingine wa kurudisha ardhi"

Leviticus 25:18

muyatii maagiza, kuzitunza sheria zangu na kuzitekeleza

Virai hivi vyote humaanisha kitu kimoja. Zinasisitiza kwamba watu wanapaswa kutii kila asemalo Yahweh.

nanyi mtakula kiasi cha shibe yenu

Hii humaanisha kwamba wangekula vya kutosha mpaka matumbo yao yajae. : "mtakuala mpaka mjazwe" au mtakula tele"

Leviticus 25:20

Labda mtasema

"Mtasema" hapa humaanisha watu wa Israeli.

Nitaiamru baraaka yangu ije juu yenu

Mungu anaiongelea baraka yake kana kwamba ilikuwa mtu amabye angeweza kumtii yeye. "Nami nitaituma baraka yangu juu yenu" au "Nami nitawabariki ninyi"

kutoka kwenye riziki iliyohifadhiwa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "kutoka katika chakula mlichohifadhi"

Leviticus 25:23

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuzungumza

Ardhi haitauzwa kwa mmiliki mpya wa kudumu,

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. ; "Haipasi kuiuza ardhi yenu kwa kudumu kwa mtu mwingine"

lazima muitunze haki ya ukomboz

Jina "ukombozi" laweza kuelezwa na vitenzi "komboa" au "nunua tena ulichokiuza." : "yawapasa mkumbuke kwamba yule mmiliki wa asili anayo haki ya kuikomboa tena ardhi wakati wowote"

itawapasa kuruhusu ardhi inunuliwe tena na familia ambayo wewe uliinunua hiyo ardhi

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "lazima muiruhusu familia ile ambayo mliinunua ardhi kwao kuinunua tena hiyo ardhi"

Leviticus 25:26

ardhi hiyo ilipouzwa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "alipoiuza hiyo ardhi"

kurejesha kwa mtu aliyemuuzia fedha iliyosalia

Hii yaweza kuwekwa wazi. : "kuilipa hiyo fedha kwa mnunuzi aliyeinunu hiyo ardhi ambayo angekuwa amishailipa"

mwaka wa Yubile

Tazama lilivyotafsiriwa katika sura 25:10

ardhi itarejeshwa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Yule aliyeinunua hiyo ardhi atairejesha"

atarejea kwenye mali yake

"atarudi kwenye ardhi yake"

Leviticus 25:29

baada ya kuuzwa

"baada ya yeye kuiuza"

haki ya ukombozi

Ile nomino "ukombozi" yawaeza kuelezwa na vitenzi "komboa" au "nunua tena ulichokiuza." : "haki ya kukikomboa"

Kama nyumba hiyo haitakombolewa

Hii yaweza kutmkkwa katika mtindo wa utendaji. : "kama yeye au familia yake hwaikomboi hiyo nyumba"

Nyumba hiyo haitakuwa ya kurejeshwa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Mtu aliyeinunua nyumba hiyo hatatakiwa kuirejesha"

Mwaka wa Yubile

Tazama livyotafsiriwa kwenye mistari iliyotangulia.

Leviticus 25:31

Lakini nyumba za vijijini zisizokuwa na ukuta

Baadhi ya vijiji havikuwa na ukuta kuvizunguka.

Zaweza kukombolewa, na ni lazima zirejeshwe

"Mnaweza kuzinunua tena nyumba mlizoziuza, na wale waliozinunua sharti wazirejeshe hizo nyumba"

mwaka wa Yubile

Tazama ulivyofafanuliwa ktika mistari iliyotangulia katika sura hii

nyumba zinazomilikiwa na Walawi katika miji yao

"zile nyumba wanazozimiliki Walawi katika miji yao"

zaweza kukombelewa wakati wowote

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Walawi wanaweza kuzikomboa wakati wowote"

Leviticus 25:33

nyumba hiyo iliyouzwa katika miji ilimo, ni lazima irejeshwe

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Yyule aliyeinunua hiyo nyuma iliyoko mjini sharti airudishe "

mwaka wa Yubile

"mwaka wa urejesho" au mwaka wa kurudisha ardhi na kuacha huru watumwa"

miongoni mwa watu wa ni mali yao

Nchi ya Kanaani iligawanywa miongoni mwa watu wa Israeli, lakini katika hiyo, Walawi walikuwa wamepewa miji 48 tu pamoja na mashamba kuizunguka miji hiyo. : "sehemu ya ardhi yao ambayo Waisraeli wanaimiliki" au "mali yao katika nchi ya Israeli"

Lakini yale mashamba yanayozunguka miji yao hayataweza kuuzwa

"Lakini Walawi hawatauza hayo mashamba yanayozunguka miji yao"

Leviticus 25:35

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuwambia Musa yawapasayo watu kutenda.

Usimtoze riba

Usimfanya akulipe zaidi ya ulichomkopesha yeye"

Leviticus 25:39

hutamfanyisha kazi kama mtumwa. Mtendee kama mtumishi wa kuajiriwa.

Hii humaanisha kwamba mmiliki alikuwa amtendee Mwisraeli kwa heshima kuliko vile ambavyo angelimtendea mtumwa.

Mwaka wa Yubile

Tazama maelezo katika 25:33

Leviticus 25:42

Maelezo Unganishi

Mungu anaendelea kumwambia Musa yaliyompasa kuwaambia watu.

wao ni watumishi wangu

"wananchi wenzako ni watumishi wangu"

Hawatauzwa kama watumwa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Haiwapasi kuwauza kama watumwa.

waweza kununua watumwa kutoka kwao.

"labda mwaweza kununua watumwa kutoka kwa mataifa hayo"

Leviticus 25:45

mgeni, -a kigeni, mpitaji

Tama maelezo katika sura zilizotangulia

Familia

Ule msemo "familia" humaanisha kikundi cha watu wanaohusiana kwa damu na kwa kawaida huhusisha baba, mama, na watoto wao. Mara kwa mara pia huhusisha ndugu wengine kama vile babu na bibi, wajuu, wajomba na shangazi. . Familia ya Kiebrania ni jamii ya kidini inayopitia chini ya mapokeo chini ya ibada na maelekezo. . Familia pia yaweza kujumuisha watumwa, masuria, na hata wageni. Baadhi ya lugha zaweza kuwa na nenonpana kama vile "ukoo" au "kaya" ambalo linaweza kufaa vema katika mazingira ambayo huhusisha zaidi ya wazazi, na watoto tu . . Ule msemo "familia" pia umetumika kumaanisha watu wanaohusiana kiroho, kama vile watu waliosehemu ya familia ya Mungu kwa sababu wanamwamini Yesu.

Watoto, mtoto

Katika Biblia ule msemo "mtoto" mara kwa mara umetuka kwa ujumla kumaanisha mtu mwingine aliye mdogo kiumri, pamoja na mtot mchanga. Ule msemo "watoto" ni mtindo wa wingi nao pia una maana nyingi za kitamathali.

. Katika Biblia, wale wanafunzi au wafuasi wakati mwingine wanaitwa "watoto" . Mara kwa mara ule msemo "watoto" limetumika kuamanisha mzao wa mtu . Kile kirai "wana wa" chaweza kumaanisha wale wanaoelezewa na kitu fulani. Baadhi ya mifano hii yaweza kuwa . watoto wa nuru . watoto wa kutii . watotowa mwovu . Msemo huu waweza pia kumaanisha watu ambao wako kama watoto wa kiroho. Kwa mfano, "watoto wa Mungu" humaanisha watu wa Mungu kupitia imani katika Yesu.

rithi, urithi, mirathi, mrithi.

Ile misemo "rithi" ana "urithi" humaanisha kupokea kitu fulani cha thamani kutoka kwa mzazi au mtu mwingine kwa sababu ya uhusiano maalum na mtu huyo. "Mrithi" ni mtu anayepokea urithi.

. Urithi wa kuonekana unaopokelewa waweza kuwa fedha, ardhi, au aina nyine ya mali. . Urithi wa kiroho ni kila kitu ambacho Mungu huwapa watu wanaoamini katika Yesu, ikiwa ni pamoja na baraka katika maisha haya pia na uzima wa mile na kukaa paoja naye.

. Pia Biblia inawaita watu wa Mungu kuwa ni hurithi wake, ambapo humaanisha kwamba wao ni wake yeye, wao ni miliki yake ya thamani.

. Mungu alimwahidi Abrahamu na wazao wake kwamba wangerithi nchi ya Kanaani, nayo ingekuwa yao milele.

. Pia kuna maana ya kitamthali au kiroho ambamo kwayo watu wa Mungu wametajwa kuwa "watairithi nchi." Hii humaanisha kwamba wao watastawi na kubarikiwa na Mungu katika njia zote mbwili kimwili na kiroro

. Katika Agano Jipya, Mungu anaahidi kwamba wale wanaomtegemea Yesu "watarithi wokovu" na "kurithi uzima wa milele." Pia imeelezwa kuwa, ni kurithi ufalme wa Mungu." Huu ni urithi wa kiroho udumuo milele. . Kuna maana nyingine za kitamathali za misememo hii

. Biblia husema kwamba wale watu wenye hekima watarithi "utukufu" na watu waliowanyoofu "watarithi mambo mema"

. "Kurithi ahadi" humaanisha kupokea mambo mema ambayo Mungu ameahidi kuwapa watu wake.

. Musemo huu pia umetumika katika maana hasi ikiwarejelea watu wapumbavu au wasiotii "watakaorithi upepo" au watakorithi "upumbavu." Hii humaanisha kwamba wanapokea matokeo ya matendo yao maovu, pamoja na adhabu maisha yasiyo na maana.

ndugu

Msemo huu "ndugu" mara kwa mara humaanisha mtu mwanaume anayeshirikiana na mtu mwingine angalau mzazi mmoja kiukoo.

. Katika Agano la Kale, msule msemo "ndugu" pia umetumika kama uhusiano wa jumla kwa jamaa kama vile washirika wa kabila, ukoo, au wa kikundi kimoja.

. Katika Agano Jipya, mara kwa mara Mitume waliutumia "ndugu" kumaanisha Mkriso mwenzako, likijumuisha wote wanaume na wanawake. kwa kuwa Waminio katika Kristo wote ni washirika wa familia moja ya kiroho, na Mungu akiwa Baba yao wa mbinguni.

. Mara chache katika Agano Jipya mitume walitumia msemo "dada" walipomaanisha Mkristo mwanamke moja kwa moja, au kusisitiza kwamba wote, wanaume na wanawake wamehusishwa. Kwa mfano, Yakobo anasisitiza kwamba anaporejelea "kaka" na "dada" anyehitaji chakula au nguo, atakuwa nazungumzia waamini wote.

MAPENDEKEZO YA UFASIRI

kikundi cha watu, watu, watu wa,

Tazama maelezo ya sura ya 18:1-3

Israeli, Waisraeli, taidfa la Israeli

Ule msemo "Israeli" in jina ambalo Mungu alimpa Yakobo, linamaana ya, "yule apambanaye na Mungu

. Wale wazao wa Yakobo walikuja kujulikana kama "watu wa Israeli," taifa la Ireaweli," au "Waisraeli."

. Mungu aliunda agano lake na watu wa Israeli. Walikuwa watu wake wateule.

. Tifa la Israeli liliundwa na makabila kumi na mbili. . Mara tu baada ya mfale Sulemani kufa, Israeli iliganyika katika falme mbili: ufalme wa Kusini uliitwa "Yuda" na ule uflamue wa Kaskazini uliitwa Israeli.

. Mara zote ule msemo "Israeli" waweza kutafsiriwa kuwa, "watu wa Israeli," au ""taifa la Israeli," kulingana tu ma mazingira.

Leviticus 25:47

baada ya Mwisraeli mwenzako kuwa amenunuliwa, anaweza kurejeshwa kwa maliopo. Mtu mwingine katika familia yake anaweza kumkomboa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Baada ya mgeni kumnunua Mwisraeli mwenzako mtu mwingine katika familia ya Mwisraeli aweza kumnunua tena aliyekuwa ameuzwa>

Leviticus 25:49

mpaka mwaka wa Yubile.

Mwisraeli angeweza kuwa mtumwa mpaka mwaka wa Yubile. Haya maelekezo ni kwa ajili ya Mwisiraeli alipotaka kuununua tene uhuru wake kabla ya mwaka wa Yubilee.

mwaka wa Yubile

Tazama maelezo katika sura zilizotangulia

kulingana na kiwango cha mendshahara anaolipwa mtumishi aliyeajiriwa

Endapo Mwisraeli anaununua tena uhuru wake, yule mgeni angeweza kukodi mtumishi ili kufanya zile kazi ambazo mwisraeli angekuwa amezifanya lakini haitakuwa hivyo. Vile vitenzi "kulipwa" na "ajiriwa" zaweza kuelezwa katika mtindo wa utendaji. : "kulingana na kiwango ambacho mtu angelipa ili kukodi mtumishi"

kwa idadi ya miaka ambayo angeweza kuendelea kufanya kazi

kwa idadi ya miaka kufikia Yubileeambayo huyo Mwisraeli angekuwa ameendelea kufanya lakini ameacha.

Leviticus 25:51

atalazimika kulipa

"huyo Mwisraeli atalazimika kurejesha"

Leviticus 25:53

:hatendewi kwa ukatili

"Huyo mgeni aliyemnunua yeye kama mtumwa itampasa kumtendea yeye."

hatendewi kwa ukali

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "hakuna amtendeaye yeye viba"

Iwapo hakukombolewa katika njia hizi

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaj, na ile naye ni lazima akombolewe kutoka yaweza kutamkwa wazi. : "Kama hayupo wa kumkomboa yeye kwa njia hizi kutoka kwa aliyemnunua kama mtumwa."

kwa njia hizi,

"katika njia hizi"

atatumika mpaka mwaka wa Yubile, yeye pamoja na watoto wake

MWisraeli mtumwa pamoja na wa watoto wake watamtumikia mgeni mpaka mwaka wa Yubile., kisha huyo Mgeni angepaswa kumwacha huru Mwisraeli huyo pamoja na watoto wake.

Kwangu mimi watu wa Israeli ni watumishi

"Kwa kuwa ni kwamba kwangu watu wa Israeli ni wa tumishi." Hii nis sababbu kwamba Mungu alitaka Waisraeli waachwe huru katika mwaka wa Yubile. Walikuwa watumishi wake. Walikuwa hawaruhusiwi kuwa wa tumwa wa mwingine wa kudumu pia.

Leviticus 26

Leviticus 26:1

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kumwambia Musa yawapasayo watu kutenda.

muzitunze Sabato zangu

"tiini sheria kwa ajili ya Sabato zangu"

Leviticus 26:3

mtatembea katika sheria zangu na kuzishika amri zangu na kuzitii

Kuna njia tatu za kuseama jambo lile lile. Yote husisitiza kwamba ni lazima watu watii kila kitu anachowaamru Mungu kufanya. "kama mtazitii kwa uangalifu sheria na amri zangu"

mtatembea katika sheria zangu

Mwenendo kulingana na sheria umezungumziwa kana kwamba ulikuwa kutembea katika sheria. : "kama mtaenenda kulingana na sheria" au "kama mtaishi kulinga na sheria zangu"

Leviticus 26:5

mtakula mkate na kushiba na kuishi

Mkate hapa huwakilisha chakula. "Hata ukamilifu" humaanisha hata matumbo yao lijazwa kwa chakula. : "mtakula chakula mpaka mmejazwa" au "mtakuwa na chakula telea chakula"

Nami nitatoa amani katika nchi

"Huko nitasababisha kuwa amani katika nchi"

upanga hautapita katika nchi yenu

Hapa "upanga" huwakilisha majeshi ya adui" au "majeshi yatawashambulieni"

Leviticus 26:7

nao wataanguka mbele yenu kwa upanga

"Kuanguka" hapa huwakilisha kufa, na "upanga" huwakilisha ama kushambulia watu kwa upanga au vita kwa ujumla"

Watu wenu watano watafukuza adui mia moja, na watu wenu mia moja watafukuza adui elfu kumi

Hii humaanisha Waisraeli watakuwa na ushindi dhidi ya majeshi makubwa.

tano ... mia moja ... elfu kumi

"5 ... 100 ... 10,000"

Leviticus 26:9

Nitawatazama kwa upendeleo

"Nitawaonyesha upendeleo" au "Nitawabariki nyinyi"

kuwafanya nyinyi mzae na kuwazidisha nyinyi

Virai hivi viwili vinamrejerelea Mungu akiwasababisha wao kuwa na wazao wengi kwa hiyo wanakuwa kundi kubwa.

kuwafanya nyinyi mzae

Mungu anakuzungumzia kuwa na watoto kwao kana kwamba walikuwa miti izaayo matunda mengi. : "nitawasababisha kuwa na watoto wengi"

Mtakula chakula kilichotunzwa ghalani kwa muda mrefu

"Mtakuwa na chakula kilichohifadhiwa ghalani cha kutosha kula kwa muda mrefu" au "Mtakuwa na chakula cha kutosha kuhifadhi ghalani na kukila kwa muda mrefu"

Leviticus 26:11

Nitaliweka hema langu katikati yenu

"Nitaweka mahali pa makao yangu miongoni mwenu"

Nami sitachukizwa nanyi

"Nitawakubali ninyi"

Nitatembea miongoni mwenu

"Nami nitawakubali ninyi"

Nimevunja makomeo ya nira yenu

Mungu anauzungumzia utumwa wao kana kwamba kulikuwa ni kuvaa nira ambayo huivaa wanyama ili kufanya kazi ngumu. Kuvunja makomeo ya nira huwakilisha kuwaweka wao huru. : "Nimewaweka huru kutoka katika kazi ngumu walizowalazimisha kuzifinya"

Leviticus 26:14

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anamwambia Musa kitakachotokea endapo watu wazitii mamri zake.

Leviticus 26:16

kama mtafanya mambo haya

Kila kirai "mambo haya" hurejelea mambo yaliyoorodheswa katika sura 26:14

Nitasababisha hofu juu yenu

Hapa "hofu" huwakilisha mambo yatakayowasababisha wao kuhofu. : "Nami nitatuma maafa yatayowaogofya ninyi"

kuondoa uhai wenu

"Nitayaondoa taratibu maisha yenu" auNitaninyi mfe pole pole" . Ni yale magonjwa na homa yatayofanya hivi.

Mtapanda mbegu zenu kwa hasara

Kile kirai "kwa hasara" humaanisha wasingepata kitu cho chote kutoka kwenye kazi zao. ; "Nanyi mtazipanda mbegu zenu bila faida" au "Nanyi mtazipanda mbegu zenu, lakini hamtapata kitu cho chote kutoka kwake"

Nitakaza uso wangu dhidi yenu

Hii humaanisha kwamba atakuwa kinyume nao. Uso wake utaonyesha ghadhabu yake naye atapigana dhidi yao.: "Nitakuwa mpinzani kwenu" au "nitakua kinyume chenu"

na mtashindwa na adui zenu

: "adui zeny watawashinda ninyi"

Leviticus 26:18

mara saba

Neno "saba" hapa siyo halisi. Humaanisha Yahweh atazidisha ukali wa adhabu yake.

Nami nitakivunja kiburi chenu

Kule kutumia nguvu lili kuwafanya wao wasiwe na kiburi kumezunguziwa kana kwamba alikuwa avunjje kiburi chao. : "Nami nitaadhibu na kwa hiyo nitakomesha kiburi unachojisikia kuusiana na nguvu zenu" na "nitawaadhibu ili kwamba msiwe na kiburi tena kwa sababu ya nguvu zenu.

Nitaifanya mbingu juu yenu iwe kama chuma na nchi yenu kama shaba

Hii humaanisaha Mungu ataizuia mvua isidondoke kutoka mawinguni. Hii itaifanya ardhi kuwa ngumu kiasi kwamba watu hawataweza kupanda mbegu au kukuza mazao.

Nguvu yenu itatumika bure

Kule kufanya kazi kwa nguvu kumezungumziwa kana kwamba kulikuwa kutumia nguvu zao ha hawa kuwa na nguvu tena. Kile kirai "bure" humaanisha kwamba wasingepata kitu kutokana na kazi kufanya kazi kwao kwa juhudi kubwa. : "Nanyi mtafanya kazi kwa juhudi sana bila mafanikio" au mtuafanya kazi kwa juhudi sana, lakini hamtapata kila kitu chema kutokana na kufanya kazi kwa juhudi sana"

Leviticus 26:21

enenda kinyume changu

Kuenenda huwakilisha tabia. Kuenenda kinyume na Mungu huwakilisha kumpinga au kumwasi Yeye. "Asi dhidi yangu"

nitaleta mapigo mara saba zaidi juu yenu

Ile nomino dhahania "mapigo" yaweza kutamkwa kama kitenzi "gonga." "Nitawagonga kwa wingi zaidi mara saba

nitaleta mapigo mara saba zaidi juu yenu

Kule Yahweh kusababisha maafa kutokea kwa Waisraeli kumezungumziwa kana kwamba angewapiga na mapigo au kuwagonga. : "Nitasabisha maafa mengi yaje mara saba dhidi yenu" au "Niitawaadhibu kwa ukali zaidi mara saba"

mara saba

Hapa "mara saba" siyo halisi, humaanisha Yahweh atazidisha ukali wa adhabu yake.

sawasawa na dhambi zenu

Ile nomino "dhambi" yaweza kuelezewa pamoja na kitenzi "tenda dhamb.i." : "kulingana na mara mlizotenda dhambi"

ambao watawaibia watoto wenu

Kuiba huwakilisha kuwavamia au kuvamia na kuwaburuta. : "watakaowavamia nyinyi na kuwaburuta watoto wenu"

Hivyo barabara zenu zitakuwa jangwa.

"Ili kwamba hatakuwepo wa kusafiri kwaenye barabara zenu." "Kuwa jangwa" humaanisha kwamba hakuna mtu yeyote huko.

Leviticus 26:23

Endapo pamoja na mambo haya

"Iwapo nitaadhibu ninyi kama hivi" au 'Iwapo nitawwadibisha ninyi kama hivi na"

msiyakubali marekebisho

Kukubali marekebisho yake huwakkilisha kuitikia kwake kwa usahihi. Katika jambo hili kuitika kwa usahihi kwake ni kuchagua kumtii Yeye. : "bado hamsikilizi marudi yangu" au "bado hamtaki kunitii Mimi"

kuenenda katika upinzani dhidi yangu

Kuenenda huwakilisha tabia. Kuenenda kinyume chake humaanisha kumpinga Yeye au kupigana dhidi Yake. : "kunipinga" au "pigana dhidi yangu"

nami pia nitaenenda kinyume chenu

Kuenenda huwakilisha tabia. Kuenenda kinyume chao humaanisha kuwapinga au kupigana dhidi yao. : "Pia Nami nitapigana dhidi yenu"

Mimi mwenyewe nitawaadhibu mara saba

Namba 7 huwakilisha ukamilifu. : "Mimi mwenyewe binafsi nitawaadhibu mara nyingi" au "Mimi mwenyewa nitawaadhibu kwa ukali wa hali ya juu"

kwa sababu ya dhambi zenu

le nomino dhambi yaweza kuelezewa na kitenzi "tenda dhambi." : "kwasababu mnaendelea kutenda dhambi dhidi yangu"

Leviticus 26:25

Nitaleta upanga juu yenu

Hapa "upanga" huwakilisha jeshi au shambulizi kutoka kwa jeshi. : "Nitaleta jeshi la adui dhidi yenu" au "nitasababisha jeshi la adui kuwavamia nyinyi"

utakaowaadhibu kwa kisasi

"amabao utawaadhibu nyinyi"

kwa sababu ya kulivunja agano

"kwa kutotii agano" au "kwa sababu hamlitii agano"

Nanyi mtakusanywa pamoja

Hii yaweza kutamkwa katika mtingo wa utendaji. : "Mtakusanyika pamoja" au "Mtajificha"

nanyi mtachukuliwa mikononi mwa adui yenu

Hapa " mikononi" humaanisha "kwenye udhibiti" na humaanisha kushindwa na adui. Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "adui zenu watawashindeni"

Nitakapokomesha mgao wa chakula,

Kule kukiharibu chakula ambacho watu wamikitunza au kuwafanya watu wasikipate kumezungumziwa kana kwamba kukata uwaji wa chakula. : "Nitakapoharibu chakula mlichokihifadhi" au "Nitakapowazuia msiweze kupata chakula"

wanawake kumi wataweza kuoka mkate wako kwenye chombo kimoja cha kuokea

Hii hudokeza kwamba kutakuwa na unga kidogo sana kiasi kwamba chombo kidogo sana cha kuokea kitaweza kubeba mikate yote ambayo wanawake wengi wateza kuweka ndani yake.

watakugawia mkate wako kwa uzani

Hii humaanisha kwamba kutakuwa na chakula kidogo sana watatakiwa kukipima ni kiasi gani kila mtu anapata.

Leviticus 26:27

Endapo hamtanisikiliza

Kusikliza huwakilisha yale aliyoyasema. : "kama hamnitii mimi"

kuenenda kinyume na mimi

Tazama maelezo katika mistari iliyotangulia katika sura hii.

nitakwenda kinyume nanyi

Tazama maelezo katika mistari iliyotangulia katika sura hii.

Nami nitawaadhibu hata mara saba

Tazama maelezo katika mistari iliyitangulia katia sura hii.

Leviticus 26:29

Nitapaangamiza ... kuziangusha ... kuzitupa maiti zenu

Kwa sababu Mungu atatuma jeshi kufanya mambo haya, anazungumzia kana kwamba atayafanya. : "Nitatuma jeshi ala adui ili kuangamiza ... kuangusha chini ... kutupa maiti zenu"

maiti zenu

"mizoga ya miili yenu"

maiti za sanamu zenu

Mungu anazungumzia sanazisizo na uhai kana kwamba zilikuwa na uhai na kisha zikafa. : "sananmu zenu zisizo na uhai"

Leviticus 26:31

Nitaigeuza miji yennu kuwa magofu na kupaharibu patakatifu penu

Kwa sababu Mungu angetuma majeshi kufanya mambo haya, anasungumza kana kwamba angeyafanya yeye mwenyewe. : "Nitatuma majeshi ya maadui ili kuigeuza miji yenu magofu na kuziharibu madhabahu zenu"

patakatifu penu

Kullikuwa na mahali ambapo watu waliabudu sanamu badala ya Mungu.

Nami sitapendezwa na harufu nzuri ya matoleo yenu

Kwa kawaida Bwana kufurahisha na harufu nzuri huwakilisha kule kufurahishwa kwake na wanaoteketeza hizo sadaka, lakini katika hili, watu wangaliteketeza sadaka zao, lakini Mungu asingependezwa nao. : "Nanyi mteteketeza sadaka zenu, lakini stapendezwa nanyi"

Nitaufuta upanga wangu na kuwafuatia

Hii huwakilisha utumaji wa majeshi ili kuwavamia. "Nitatuma majeshi ya maadui ili kuwashambulia nyinyi" au "Nitatuma majeshi ya maadui ili kuwashambulia nyinyi kwa mapanga"

Nchi yenu itatelekezwa, na miji yenu itakuwa magofu

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "nany mtaitelekeza nchi yenu , nao adui zenu wataiharibu miji yenu"

Leviticus 26:34

Nayo nchi itazifurahia Sabato zake

Hao watu walipaswa kuitii sheria ya Sabato kwa kutoilima ardhi kila mwaka wa saba. Mungu anazungumzia juu ya hili kana kwamba ardhi ilikuwa mtu ambaye angalitii sheria ya Sabato na kupuzika. : "Kisha nchi itapumzika kulingana na sheria ya Sabato" au "Kisha, kama inavyotakiwa na sheria ya Sabato, ardhi haitalimwa"

nchi itapumzika

Mungu huzungumzia juu ya nchi kutolimwa kana kwamba alikuwa mtu ambaye angepumzika, : "haitalimwa"

Nitatuma hofu ndani ya mioyo yenu

Kutuma hofu myoyoni mwao huwakilisha kuwafanya wao waogope"

kana kwamba mlikuwa mkikimbia mbele za upanga

Upanga huwakilisha ama mtu mwingine aliyekuwa tayari kuua akitumia upanga au shambuzi kutoka kwa jeshi la adui. : "kana kwamba mlikuwa mkitoroka mtu mwingine aliyekuwa akiwafukuza na upanga" au kana kwamba mlikuwa mkilitorka jeshi la adui"

Leviticus 26:37

Taarifa kwa Ujumla

Yahweh anaendelea kuelezea kitachotokea kwa Waisraeli watakapolazimisha kwenda mataifa ya adui zao.

kana kwamba mlikuwa mkiukimbia upanga

Tazama maelezo kuhusu upanga na uwakilishi wake katika mistari iyotangulia

kusimama mbele za aduii zenu

Kusimama mbele za adui huwakilisha kuanguka adui wanawapovamia na kupigana dhidi yao. : "kuwazuia adui zenu wanawavamia ninyi" au "kujibu mapigo dhidi ya adui zenu"

nayo nchi ya adui zenu yenyewe itawamezeni

Yahweh anaongelea kuhusu nchi ya maadui kana kwamba ilikuwa mnyama pori ambaye angewala Waisraeli. Lile neno "meza" husisitiza kwamba wengi wa Waisraeli watafia huko. : "matfia katika nchi ya adui zenu"

Wale watakosalia miongoni mwenu

"Wale wa kwenu ambao wasiokufa"

wataangamia katika dhambi zao

Kuangamia katika dhambi zao huwakilisha kuangamia kwa sababu ya dhambi zao.

dhambi za baba zao

Hapa "za baba zao" huwakilisha wababu wao

Leviticus 26:40

kugeuka dhidi yao

Hii huwakilisha kuwapinga> : "kuwapinga wao"

iwapo mioyo yao isiyotahiriwa itanyenyekezwa

Hapa ule msemo "mioyo isiyotahiriwa" humaanisha nafsi nzima. : " kama wao watakuwa wanyenyekevu badala ya kukaidi kwa ushubavu"

nami nitalikumbuka agano langu na Yakobo, agano langu na Isaka, agano langu na Abrahamu

"Kukumbuka " ni nahau inayomaanisha kukumbuka kwa makusudi. Hapa inawakilisha kutimiza agano lake. : "kisha nitatimiza agano nililofanya na Yakobo, Isaka na Abrahamu"

nitaikumbuka nchi

"Kukumbuka " ni nahau inayomaanisha kukumbuka kwa makusudi." Hapalinawakilisha nchi. : "Nitatimiza ahadi yangu juu ya nchi"

Leviticus 26:43

Nayo nchi itakuwa imetelekezwa na wao

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Watu wa Israeli waitelekeza nchi yao"

Leviticus 26:44

nitalikumbuka agano langu na baba zao

: "Nitatimiza agano langu na babu zao.

Maelezo kwa Ujumla

Hili lina hitimisha ujumbe wa Yahweh kwa Musa katika mlima wa Sinai kuhusiana na baraka kwa utii na adhabu kwa kutotii.

machoni pa mataifa

Hii huwakilisha ufahamu wa mataifa. ": "katika ufahamu wa mataifa" au "nayo mataifa yajue kuhusu hili"

mataifa

Hili huwakilisha watu wa mataifa. "machoni pa watu wa mataifa"

Leviticus 26:46

amru, kuamru, amri

Ule msemo "amru" humaanisha kumwagiza mtu mwingine kufanya jambo fulani. "Agizo" au "amri ni kile mtu aliagizwa kufanya.

. Ingawaje misemo hii yote inamaana moja kimsingi, maraa kwa mara "amri" hurejelea maagizo fulani ya Mungu amabayo yako rasmi zaidi na ya kudumu, kama vile "amri kumi"

. agizo laweza kuwa chanya ("Heshimu wazazi wako") au hasi ("Usiibe")

. "Kuchukua amri" humaanisha "kuchukua udhibiti" au "shika madaraka" ya kitu kitu fulani au mtu mwingine.

Agizo

Agizo ni tangazo au sheria amabayo hutangazwa hadharani kwa watu wote. . Sheri za Mungu pia huitwa maagizo, masharti au amri. . kama vile sheria na amri, maagizo lazima yatiiwe

. Mfano wa agizo lililotolewa na mtawala mwanadamu ni lile tangazo lililotolewa na Kaisari Augusto kwamba kila aliyekuwa akiishi katika Dola la Kirumi lazima arudi katika mji wa nyumbani kwao apate kuhesabiwa kwenye sensa.

. Kuagia kitu fulani humaanisha kutoa amri ambayo lazima itiiwe. Hii ingeliweza kutafsiriwa kama, "kuagiza" au "kuamru" au "kudai kirasmi" au kutengeneza sheria hadharani."

. Jambo fulani "lililotangazwa" kutokea humaanisha kwamba hakika hili litatokea. au lililokwisha kusudiwa na halitabadilishwa" au "limetangazwa kabisa kabisa kwamba litatokea."

sheria, sheria ya Musa, sheria ya Mungu, sheria ya Yahweh

Misemo hii yote hurerjea amri na mfundisho ambayo Mungu alimpa Musa kwa ajili ya Waisraeli kuzitii. Ile misemo "sheria" na sheria ya Mungu" kwa ujumla pia imetumika kumaanisha kila kitu ambacho Mungu anawatakawatu wake kutii. . Kwa kutegemeana na muktadha, sheria yaweza kumaanisha: . zile amri kumi ambazo aliziandika kwenye mbao za mawekwa ajili ya Waisraeli. . sheria zote alizopewa Musa . vile vitabu vitano vya kwanza vya Agano la Kale. . Agano la Kale lote (pia hurejelewa kama "maandiko" katika Agano Jipya. . Mafundisho yote na maenzi ya Mungu . Kile kirai" sheria na manabii" katika Agano Jipya kimetumika kumaanisha maandiko ya Kiebrania (Agano la Kale)

Sinai, Mlima Sinai

Mlima sSinai ni jina la mlima ambao huenda kulikuwa upande wa eneo linaitwa kwa sasa rasi ya Sinai. Pia lilijulikana "Mlima Horebu." . Mlima Sinai ni sehemu kubwa ya jangwa lenye miamba. Waisraeli walikuja kwenye Mlima Siani walipokuwa wakisafiri kutoka Misri kwenda kwenye Nchi ya Ahadi. . Mungu alimpa Musa zile amri kumi juu ya Mlima Siani

Leviticus 27

Leviticus 27:1

Iwapo mtu yeyote anatoa kiapo maalum cha kuwa mnathiri kwa Yahweh

Katika jambo hilikiapo kingehusisha kujito mwenyewe au mtu mwingine kwa Mungu. Hii yaweza kutamkwa wazi. : "Kiwa mtu fulani anaapa kmtoa mtu mwingine kwa Yahweh"

tumieni tathmini zifuatazo

Badala ya kumpa mtu, yeye ndiye angempa Bwana kiasi fulani cha cha fedha. : "Tumieni thamani fulani kama zawadi yenu kwa Bwana kwanya nafasi ya mtu" au mpeni Bwana kiasi kifuatacho cha fedha badala ya mtu"

Leviticus 27:3

tumieni tathmini zifuatazo viwe viiwango vyenu vya thamani

"Kiasi cha kulipa" au yapasa ulipe"

Ishirini ... sitini ... hamsini ... thelathini

"20 ... 60 ... 50 ... 30"

shekeli hamsini za fedha

Kama ni laziam kutumia vipimu vya uzani vya kisasa, hapa kuna nhia mbili kufanya hilo. "vipand hamsini vya fedha, ambacho kila kimoaja hupima gramu kumi" au "gramu mia tano za fedha"

kulingana na vipimo vya shekeli ya mahali pa patakatifu

Hizi zikikuwa shekeli za vipimo mbali mbali. Hii ni njia moja ambayo mtu alikuwa atumie kwenye hema takatifu. Kilipima gramu 11. : Tumie aina ya shekeli inayotumika kwenye hema la kukutania" au "mnapopima fedha, tumieni ni kipimo amabacho hutumika kwenye hema.

shekeli thelathini

: "vipande thelathini vya fedha, ampao kila kimoja hupima gramu kumi" au "shekeli thelathini sawasawa na gramu mia tatu"

Leviticus 27:5

tano ... ishirini ... kumi ... tatu

"5 .. 20 ... 10 ... 3"

viwango vyenu

"kiasi cha kulipa' au yapasa mlipe"

shekeli ishirini

: "vipande ishirini vya fedha" au "gramu mia mbili za fedha"

na kwa mwanamke ni shekeli kumi

Kirai "umri huo" na "viwango vyenu vya thamani vitakuwa" ni vimeachwa wazi viweze kuelekweka. : "naye mwanamke wa umri huo lazima viwango vyenu vya thamani viwe shekeli kumi"

shekeli kumi

"vipande kumi vya fedha" au gramu hamsini za fedha"

shekeli tano za fedha

"vipande vitano vya fedha" au gramu mia moja za fedha"

shsekeli tatu

"vipande vitatu vya fedha" au gramu thelethini za fedha"

Leviticus 27:7

miaka sitini na zaidi

"umri wa miaka sitini na wazee"

Sitin ..kumi na tano .. kumi

"60 ... 15 ... 10"

shekeli kumi na tano

"vipande kumi na tanovya fedha" au "gramu 150 za fedha"

huyo mtu anayetolewa lazima atapelekwa kwa kuhani

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "atampeleka kwa kuhani huyo mtu anayemtoa"

Leviticus 27:9

atatengwa kwake.

"atangwa kwa Yahweh"

hao wawili; yule anayetolewa na yule anayebadilishwa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "wote wawili huyo aliyetolewa na yule anayembadilisha" au " mnyama naweza kumaanisha kuwa "wanyama wote wawili"

Leviticus 27:11

kwa uhalisia siyo kisafi, kwa hiyo, Yahweh hatakikubali

Mnnyama amezungumziwz kana kwamba alikuwa mchafu kimaumbbile. Anaweza kuwa najisi kwa sababu ni anina fulni ya mnyama au kwa sababu ana kasoro. .: kwa uhalisia ni yule ambaye Yahweheh hatampokea"

thamani ya soko

Hii ni thamani ambayo mnyama huwa thamani tu anamnunua au kumuuza.

anapenda kumkomboa

anapena kumrejesha kwa kumnunua tena"

Leviticus 27:14

atalazimika kuongeza sehemu ya tano ya thamani yake kwenye gharama ya

"ya tano ni sehemu ya kitu fulani iliyowanywa katika sehemu tano zilizo sawa kwa kila moja ya sehemu hizo, na kuilipa yote"

Leviticus 27:16

kiasi cha mbegu inayotakiwa kuipanda katika ardhi hiyo

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "kile kiasi cha mbegu mtu angehitaji kupanda"

homeri moja ya mbegu za shairi ambayo itathamanishwa

Hapa "homeri moja ya shayiri huwakilisha kipande cha ardhi ambaho kingehitaji homeri moja ya shaiyiri ili kupandwa chote. : "kipanda cha ardhi kinachohitaji kudhamanishwa kwa homeri moja ya shayiri ili kuweza kupandwa chote" au " Thamani ya ardhiinayohitaji homeri moja ya shayiri itatakiwa"

homeri

homeri moja ni lita 220

shekeli hamsini za fedha

"vipande hamsini vya fedha , ambavyo kila kimoja bgramu kumi" au " gramu mia tano za fedha"

Leviticus 27:17

mwaka wa Yubile

Tazama maelezo ya sura 25:10

tathmini yake ya awali itabaki kuwa ileile

au "thamani yake itakuwa bei kamili

thamani yake lazima ishushwe.

"itamlazimu kupunguza thamani iliyokadiliwa"

Leviticus 27:19

haliwezi kukombolewa tena

Hii yaweza kumtakwa katika mtindo wa utendaji. : "hawezi kulirejesha kwa kulinunua tena"

Iwapo halikomboi shamba

Ule muda wa kukomboa shamba waweza kutamkwa wazi. : kama halikomboi shamba kabla ya mwak wa Yubile"

katika mwaka wa Yubile

AngTazama amaelezo ya sura ya 25:13

shamba lililotolewa kabisa kwa Yahweh

Hii yaweza kumtakwa katika mtindo wa utendaji. : "ambalo mtumwingie kalitoa kabisakabisa kwa Yahweh"

Leviticus 27:22

tenga

Ule msemo "tenga" humaanisha kutengwa kutoka kwenye kitu fula ili kutimiza kusudi fulani. . Waisraeli walitengwa kawa ajili ya huduma kwa Mungu. . Roho Mtakatifu aliwaagiza Wakristo huko Antiokia kuwatenga Paulo na Barnaba kwa kazi ambayo Mungu aliwataka wao waifanye . Mwamini "aliyetengwa" kwa ajili ya huduma kwa Mungu "kwakifishwa" kutimiza mapenzi ya Mungu. . maana mojawapo ya msemo "mtkatifu" ni kutengwa kuwa Mungu na kuwa umetengwa kutokanjia za dhambi za ulimwengu. . Ule msemo "takasa" humaanisha kutenga mtu kwa ajili ya huduma ya Mungu.

Leviticus 27:24

mtu yule ambaye lilikuwa limenunuliwa ... mmiliki wa ardhi

Virai hivi viwili humrejelea mtu yule yule. Kwa kawaida ardhi ingenunuliwa kutoka kwa mmiliki wake.

mtu yule ambaye lilikuwa limenunuliwa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "mtu aliyeliuza"

Tathmani yote lazima ifanywe

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "kuahani ataamua ukadiliaji wa thamani"

kwa uzani wa shekeli ya mahali pa patakatifu

Kulikuwa na shekeli za vipimo mbali mbali. Hiki kilikuwa ni kimojawapo ambacho watu ilikuwa watumie ndani ya hema takatifu.

Gera ishirini kwa shekeli moja.

Kusudi la sentensi hii ni kutamka ni kiasi gani shekeli ya patakatifu hupimwa. Gera ilikuwa ni uzani mdogo sana wa kipimo walichotumia Waisraeli: "Sharti shekeli moja iwe sawasawa na gera ishirini"

Gera ishirini kwa shekeli moja.

: "Shekeli moja yapasa ipime gramu kumi"

Leviticus 27:26

Asiwepo mtu atakayetenga

Hakuna awezaye kutenga kwa ajili ya Yahweh"

sehemu ya tano lazima itaongezwa kwenye thamani hiyo

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "naye atalzaimika kuongeza moja ya taon kwenye thamani hiyo"

Na kama mnyama hakombolewi

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Kama mtu hamtejeshi kwa kumnunua tena huyo mnyama"

naye atauzwa kwa thamani iliyowe

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji : "kuhani atamuuza kwa thamani iliyowekwa"

Leviticus 27:28

Hakutakuwa na kitu amabacho mtu anakitoa kwa Yahweh, kutoka katika vyote alivyonavyo, iwe ni mwanadamu au mnyama, au ardhi ya familia yake, ambacho chaweza kuuzwa au kukombolewa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Hukuna wawezaye kuuza au kukomboa kitu chochote mtu alichokitoa kwa Yahweh, kutoka katika vyote alivyonavyo, ama awe ni mwanadamu, mnyama, au ardhi ya familia yake", au "iwapo mtu amatoa kwa Yahweh kitu chochote alichonacho, ama awe mwanadamu au mnyama, au ardhi ya familia yake, hatakuwapo mtu anaweza kukiuza au kukikomboa"

Kila kitu kitolewacho ni kitakatifu sana kwa Yahwe

"Kila kitu mtu akitoacho ni kitakatifu sana kwa Yahweh"

Hakuna fidia inayoweza kulipwa

"hakuana akuwezaye kulipa fidia"

kwa kuwa mtu aliyelitolewa kwa ajili ya uangamizwa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "kwa kuwa mtu yeyote ambaye Yahweh kamtoa kwa ajili ya uangamivu"

Mtu huyo lazima auawe

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "lazima mmuue mtu huyo" au "yawapasa kumuua mtu"

Leviticus 27:30

Iwapo mtu anakomboa chochote cha zaka yake

Kama mtu anataka kurejesha tena zaka yake kwa kuinunua"

Leviticus 27:32

yeyote anayepita chini ya fimbo ya mchungaji

Hii hurejea njia ambayo wangehesabu wanyama wao. : "unapohesabu wanyama wwako kwa kuinua fimbo ya mchungaji wako na huku wakipita chini ya fimbo hiyo kwenda upande mwingine" au "munapowahesabu wanyama"

wa kumi mmoja lazima atengwe kwa ajili ya Yahweh

wakumi lazima atengwe kwa ajili ya Yahweh - sentensi yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "yawapasa mumtenge wa kumi mmoja kwa ajili ya Yahweh"

mmoja wa kumi

ya kumi- "kila mnyama wa kumi"

kisha wote wawili yule wa kwanza na huyo aliyebadiliwa

"kisha wanya wote wawili"

hawezi kukombolewa

Hii yaweza kutamkwa katika mtindo wa utendaji. : "Hataweza kumkomboa" au "Hataweza kummrejesha kwa kumnunutena"

Leviticus 27:34

Hizi ndizo amri

Huu ndiyo Mhitasari wa maelezo. Hurejerea zile amri zilizotolewa kwenye sura zilizotangulia.

Numbers 1

Numbers 1:1

Siku ya kwanza ya mwezi wa pili

Huu ni mwezi wa pili wa kalenda ya Kihebrania. Siku ya kwanza iko karibu na katikati ya mwezi wa Aprili kwa kalenda ya nchi za Kimagharinbi.

Mwaka wa pili

"Mwaka wa 2"

Wahesabu kwa majina

Kuwahesabu wanaume kwa kunakiri majina yao.

Umri wa miaka ishirini

"Umri wa miaka 20"

Unakiri majina ya wanaume kwa katika makundi yao ya kijeshi

Kuwaandika wanaume kufuata vikosi vya kijeshi.

Numbers 1:4

Kichwa cha ukoo

"kiongozi wa ukoo"

Kutumika pamoja na wewe

"kukusaidia"

Elizuri ... Shedeuri ... Shelumieli ... Zurishadai

Haya ni majina ya wanaume.

Numbers 1:7

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kumtajia Musa orodha ya majina ya viongozi wa makabila.

Numbers 1:10

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kumtajia Musa orodha ya majina ya viongozi wa makabila.

Numbers 1:12

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kumtajia Musa orodha ya majina ya viongozi wa makabila.

Numbers 1:16

Wale wanaume waliokuwa waliokuwa wameandikwa.

"Wale wanaume ambao BWANA amewchagua"

Numbers 1:17

Wakawachukua wale wanaume

"Wakawakusanya wale wanaume pamoja"

Waliokuwa wameandikwa kwa majina

"Ambao majina yao walikuwa wameyaandika"

Siku ya kwanza ya mwezi wa pili

"Siku ya 1 ya mwezi wa 2." Huu ni mwezi wa pili wa kalenda ya Kihebrania. Siku ya kwanza iko karibu na siku ya katikati ya mwezi wa Apili katika kalenda ya kimagharibi.

Kishsa kila mwanamume ... alitambua babu zake. Alitakiwa kutaja koo na familia kutoka katika ukoo

Sentensi ya pili inafanana na sentensi ya kwanza ila imetumika kuongeza ufafanuzi.

Alitakiwa kutaja

"Kutaja" inamaanisha "kusema." "Kila mwanamume alitakiwa kusema"

Numbers 1:20

Yalihesabiwa majina yote

"waliheabau majina yote"

wenye uwezo wa kwenda vitani

"waliokuwa na uwezo wa kwenda viatani"

wanaume 46,500

"wanaume elfu arobaini na sita, n a mia tano"

Numbers 1:22

yalihesabiwa majiina yote ya kila mwanamume ... ya ukoo na familia

Tazama 1:20

Numbers 1:24

yalihesabiwa majiina yote ya kila mwanamume ... ya ukoo na familia

Tazama 1:20

Numbers 1:26

yalihesabiwa majiina yote ya kila mwanamume ... ya ukoo na familia

Tazama 1:20

Numbers 1:28

yalihesabiwa majiina yote ya kila mwanamume ... ya ukoo na familia

Tazama 1:20

Numbers 1:30

yalihesabiwa majiina yote ya kila mwanamume ... ya ukoo na familia

Tazama 1:20

Numbers 1:32

yalihesabiwa majiina yote ya kila mwanamume ... ya ukoo na familia

Tazama 1:20

Numbers 1:34

yalihesabiwa majiina yote ya kila mwanamume ... ya ukoo na familia

Tazama 1:20

Numbers 1:36

yalihesabiwa majiina yote ya kila mwanamume ... ya ukoo na familia

Tazama 1:20

Numbers 1:38

yalihesabiwa majiina yote ya kila mwanamume ... ya ukoo na familia

Tazama 1:20

Numbers 1:40

yalihesabiwa majiina yote ya kila mwanamume ... ya ukoo na familia

Tazama 1:20

Numbers 1:42

yalihesabiwa majiina yote ya kila mwanamume ... ya ukoo na familia

Tazama 1:20

Numbers 1:44

Kwa hiyo wanaume wote wa Israeli ... walihesabiwa kutoka kwenye familia zao

Tazama 1:20

Numbers 1:47

wanaume toka ukoo wa Lawi hawakuhesabiwa

"Musa na Haruni hawakuwahesabu wale wanaume waliokuwa wakitoka ukoo wa Lawi

waliokuwa wakitoka ukoo wa Lawi

"waliokuwa wakitoka kwenye kabila la Lawi

usiwahesabu wale wa kabila la Lawi

"kabila la Lawi" inamaanisha wanaume wote wa akbila la Lawi". "usiwahesabu wanaume wote wa kabila la Lawi"

Numbers 1:50

Hema la amri za agano

Lile hema pia lilitwa kwa jina hili kwa sababu lile sanduku lenye sheria liliwekwa ndani yake.

vyote vilivyomo

Neno "mo" inamaanisha masikani

Walawi watalazimika kuibeba masikani

Mtakaposafari, Walawi wataibebba masikani

Kuzitengeneza kambi zinazoizunguka

Wataweka kambi zao kuizunguka.

Numbers 1:51

Na kila hema litakapotakiwa kusimamishwa

"wakati wa kuisimamisha masikani utakapofika"

Na mgeni ... atauawa

"Mtamwua kila mgeni atakayeisogelea masikani"

bango

bendera kubwa

jeshi lake

"kikosi chake cha kijeshi"

Numbers 1:53

Masikani ya amriza agano

Tazama 1:50

Ili kwamba hasira yangu isije ikawaka juu ya wana wa Israeli

"ili kwamba katika hasira yangu nisije nikawaadhibu watu wa Israeli"

BWANA aliagiza kupitia Musa

BWANA alikuwa amemwagiza Musa mambo yote ambayo Waisraeli walipaswa kufanya, na ndipo Musa alipowaagiza Waisraeli.

Numbers 2

Numbers 2:1

kulingana na mahali pake

Kulikuwa na makundi makubwa manne ambayo makabila yalikuwa yamegawanyika. Kila kundi liliamuliwa kukaa mahali pamoja. Kila kundi lilitambulishwa na bango.

pamoja na mabango ya baba zao

Kila ukoo ulikuwa na bango lao hapo kambini, ambalo lilikuwa ndani ya eneo kufuata mahali pao.

mabango

bango ni bendera kubwa.

Numbers 2:3

katika kuundi lao

Tazama 2:1

Nashono mwana wa Aminadab

Tazama 1:7

74,600

"elfu sabini na nne, na mia sita.

Numbers 2:5

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaenedelea kumwambia Musa mahali ambapo kila kabila na jeshi lao litakapoweka kambi kuizunguka hema ya kukutania.

Nathaniel mwana wa Zuari

Tazama 1:7

Kikosi

Hili ni neno la kijedshi lenye maana ya kundi kubwa la wanajeshi. Kila kabila lilikuwa na "kikosi chake."

Numbers 2:7

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaenedelea kumwambia Musa mahali ambapo kila kabila na jeshi lao litakapoweka kambi kuizunguka hema ya kukutania.

Eliabu mwana wa Heloni

Tazama 1:7

57,400

wanaume 57,400

Numbers 2:9

Idadi yote ya kambi ya Yuda ni 186,400

Idadi hii inajumuisha wanaume wote katika makabila ambayo yalikuwa yameweka kambi kufuata mahali pa Yuda. "Idadi ya wanaume waliokuwa wameweka kambi ya Yuda ni 186,400.

Watakuwa wa kwanza kuondoka

Hii inamaanisha kuwa watakuwa wa kwanza wakati kambi za Waisraeali zitakapoondoka. "Wakati wa kusafiri watakuwa wa kwanza kuondoka.

wa kwanza

"wa 1"

Numbers 2:10

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaenedelea kumwambia Musa mahali ambapo kila kabila na jeshi lao litakapoweka kambi kuizunguka hema ya kukutania.

Katika kundi lao

Tazama 2:1

Elizuri mwana wa Shedeuri

Tazama 1:4

46,500

"wanaume 46,500"

Numbers 2:12

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaenedelea kumwambia Musa mahali ambapo kila kabila na jeshi lao litakapoweka kambi kuizunguka hema ya kukutania.

Shelumieli mwana wa Zurishadai

Tazama 1:4

59,300

"wanaume 59,300

Numbers 2:14

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaenedelea kumwambia Musa mahali ambapo kila kabila na jeshi lao litakapoweka kambi kuizunguka hema ya kukutania.

Eliasafu mwana wa Deuli

Tazama 1:12

45,650

"wanaume 45,650"

Numbers 2:16

Wote waliohesabiwa kwenye kambi ya Reubeni, kulingana na vikosi vyao, ni 151,450

Idadi ya wanaume wote waliokuwa wameweka kambi mahali pa Reubeni kwa kufuata vikosi vyao ni 151,450"

wa pili

"wa 2"

Numbers 2:17

hema ya kukutania kuondoka kambini .. katikati ya kambi zote

Hii inamaanisha kuwa hema ya kukutania lazima libebwe na Walawi katikati ya makabila wakati wa safari.

Lazima waondoke

neno "wa" inamaanishsa makabila kumi na mbili.

kwa kufuata bango lake

"Kwa bango la kabila lake"

Numbers 2:18

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaenedelea kumwambia Musa mahali ambapo kila kabila na jeshi lao litakapoweka kambi kuizunguka hema ya kukutania.

Kufuata mahali pao

Tazama 2:1

40,500

wanaume 40,500

Numbers 2:20

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaenedelea kumwambia Musa mahali ambapo kila kabila na jeshi lao litakapoweka kambi kuizunguka hema ya kukutania.

Baada ya hao

Hii inamaanisha kuwa kabila na Manase ndilo litakalofuatia.

32,200

wanaume 32,000

Numbers 2:22

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaenedelea kumwambia Musa mahali ambapo kila kabila na jeshi lao litakapoweka kambi kuizunguka hema ya kukutania.

Kabila litakalofuata

Hii inamaanishsakuwa kabila la Manase ndilo litakalofuata, baada ya kabila la Efraimu.

35,400

Wanaume 35,400

Numbers 2:24

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaenedelea kumwambia Musa mahali ambapo kila kabila na jeshi lao litakapoweka kambi kuizunguka hema ya kukutania.

Wote waliohesabiwa katika kambi ya Efraimu ni 108,100

Idadi ya wanaume waliokuwa wameweka kambi mahali pa Efraimu ni 108,100.

wa tatu

"wa 3"

Numbers 2:25

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaenedelea kumwambia Musa mahali ambapo kila kabila na jeshi lao litakapoweka kambi kuizunguka hema ya kukutania.

kambi ya kikosi cha Dani

Hii inamaanisha kikosi kizima cha Dani, Asheri, na Naftali ambao wako mahali pa Dani. "Kikosi ambacho kinaweka kambi mahali pa Dani.

Ahiezeri mwana wa Amishadai

Tazama 1:12.

62,700

Wanaume 62,700

Numbers 2:27

Taarifa kwaujumla

BWANA anaenedelea kumwambia Musa mahali ambapo kila kabila na jeshi lao litakapoweka kambi kuizunguka hema ya kukutania.

PAgieli mwana wa Okirani

Tazama 1:12

41,500

Wanaume 41,500

Numbers 2:29

Taarifa kwaujumla

BWANA anaenedelea kumwambia Musa mahali ambapo kila kabila na jeshi lao litakapoweka kambi kuizunguka hema ya kukutania.

Ahira mwana wa Enani

Tazama 1:12

53,400

Wanaume 53,400

Numbers 2:31

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaenedelea kumwambia Musa mahali ambapo kila kabila na jeshi lao litakapoweka kambi kuizunguka hema ya kukutania.

Wote waliohesabiwa kwenye kambiya Dani walikuwa 157,600

"Idadai ya wanaume waliohesabiwa kwenye kambi ya Dani ni 157.600

Numbers 2:32

wote waliohesabiwa

Musa na Haruni waliwahesabu wote

kwa kufuata vikosi vyao

Neno "vyao" inamaanisha wana wa Israeli

Numbers 2:34

Walisafiri kutoka kambini

"Waliposafiri waliondoka kambini"

Numbers 3

Numbers 3:1

Sasa

Mwandishi analitumia neno "sasa" ili kuonyesha anavyoanza kueleza habari nyingine.

Nadabu, mzaliwa wa kwanza

"Nadabu, aliyekuwa mzaliwa wa kwanza"

Nadabu ... Abihu ... Ithamari

Haya ni majina ya wanaume

Numbers 3:3

Wale makuhani waliokuwa wametiwa mafuta na kuwekwa wakfu.

"wale makuhani ambao Musa aliwatia mafuta na kuwaweka wakfu"

Nadabu ... Abihu ... Ithamari.

Tazama 3:1

walikufa mbele za BWANA

Kirai cha "walikufa" kinamaanishsa kufa ghafula. "Walikufa ghafula mbele za BWANA"

Mbele za BWANA

iNamaanisha uwepo wa BWANA, kwa maana ya kwamba BWANA aliona kila kitu kilichokuwa kikitokea. Au "Katika uwepo wa BWANA"

Walipomtolea moto usiokubalika

Neno "moto" limetumika kumaanisha "uvumba wa kufukiza." Walichoma uvumba wa kufukiza ambao BWANA hakuukubali."

Numbers 3:5

Walete kabila ya Lawi

Hapa neno "kabila" inamaanisha wanaume walio katika kabila hiyo

Numbers 3:7

badala ya

"kwa." Hii inamaanisha kufanya kazi ya mwingine kama mwakilishi wa wengine.

watayatumikia makabila ya Israeli

Hapa "makabila ya Israeli inamaanisha watu wa Israeli. "Kuwatumika watu wa Israeli"

watawatumikia makabila ya Israeli kwa huduma ya hemani

Kirai cha "kwa huduma" kinamaanisha kutumika." "Wtawasaidia Waisraeli kwa kutoa huduma ya hemani"

kwa huduma ya hemani

"kazi ya hemani."

Numbers 3:9

Uwaweke

"U" inammaanisha Musa.

Nimewatoa kikamilifu

Nimewatoa kwa vyote

mgeni yeyote atakayekaribia lazima auawe

"lazima mmuue mgeni yeyote atakayesogea karibu.

lakini mgeni yeyote atakayekaribia

"lakini mgeni yeyote atakayeikaribia masikani"

Numbers 3:11

Tazama

"Sikiliza" au "Uwe msikivu kwa kile ninachotaka kukuambia"

Nimewachukua Walawi

"Nimewachagua Walawi"

Numbers 3:14

Wahesabu uzao

"Wahesabu wazao wa kiume"

katika nyumba za koo zao

Neno "nyumba za koo zao" linamaanisha "wazao wa ukoo" nineno lingine lenye maana ya koo zao." au kwa kufuata koo zao.

Kufuata maelekezo ya BWANA, kama alivyoamriwa kufanya.

Kimsingi virai hivi viwili vinamaanisha kitu kilekilke na vimetumika pamoja ili kutia msisitizo kuwa alimtii BWANA.

Numbers 3:17

Taarifa kwa ujumla

Hii ni orodha ya uzao wa Lawi

Ukoo uliotokana na

Hapa mwandishi anamaanisha ukoo "unaotoka" kwa

Numbers 3:21

Zilitokana na Gerishoni

Hapa mwandishio anatumia neno "kutokana" na kuonyesha kama unaotoka kwa. "Zinatoka kwa Gerishoni"

Walibini ... Washimei ... Wagerishoni

Walibini n a Washimei ni majina ya koo waliotajwa kwa kufuata vichwa vya familia zao. Wagerishoni ni jina la watu wanaotokanana Gerishoni.

Wanaume wote wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi walihesabiwa

Musa aliwahesabu wanaume wote kuanzia wenye umri wa mwezi mmoja na zaidi.

7,500

elfu saba na mia tano

Numbers 3:24

Elisfu ... Laeli

Haya ni majina ya wanaume

Lile pazia la lango

"pazia la kwenye ua"

ua unaozunguka mahali patakatifu na madhabahu

"huo ni ua unaozunguka mahali patakatifu na madhabahu"

Numbers 3:27

Taarifa kwa ujumla

Hii niorodha ya koo zilizotokana na Kohathi

Kohathi

Tazama 3:17

Wanaume 8,600 walihesabiwa

Musa aliwahesabu wanaume 8,600

wenye umri wa mwezi mmoja na zaidi

"Kuanzia mwenzi mmoja na zaidi"

Numbers 3:30

Taarifa kwa ujumla

Mistari hii inatupatia taarifa zinahusiana na koo ambazo zinatokana na Kohathi.

vitu vitakatifu ambavyo hutumika katika huduma yao

"vitu vitakatifu ambavyo makuhani hutumia katika huduma"

Numbers 3:33

Taarifa kwa ujumla

Hii ni orodha ya ukoo u naotokana na Merari

Wanaume 6,200 walihesabiwa

"Musa aliwahesabu wanaume 6,200"

Numbers 3:36

Mbao za hema

Hizi ni mbao zinazotenegenezwa kwa kuunganisha vipande viwili vya mbao.

mataruma

Hii ni mihimili inayolifanya jengo kuwa na imara.

nguzo

Nguzo ni ubao imara unaosimamishwa wima ili kushikilia kitu.

makalishio

hivi ni vitu ambavyo viliwekwa mahali ambapo nguzo zilisimikwa.

vifaa vya ujenzi

Hii inamaanishsa kila kitu ambacho kilitumika kwa kuunganishia mataruma, nguzo na makalishio

pamoja na vigingi vyake

kiwakilishi "vyake" inamaanisha mihimili na nguzo.

vitundu, vigingi na kamba zake

Hivi ni vifaa ambavyo vilitumika ili kuunganisha mbao zilizolazwa kwenye nguzo.

Numbers 3:38

watoto wake

Neno "wake" inamhusu Haruni

kuelekea mawio ya jua

huu ni upande wa mashariki wa masikani. "upande ule wa mashariki kwenye mawio ya jua"

wataajibika na majukumu

neno "majukumu" ni nomino zahania inayoweza kuelezeka kama kitenzi, "kufanya majukumu"

mgeni atakayekaribia mahali patakatifu auawe"

Utamwua kila mgeni atakayekaribia mahali patakatifu

wanaume ishirini na mbili elfu

wanaume 22,000

Numbers 3:40

utwae wanyama wa Walawi

"utanitwalia wanyama wote wa Walawi.

Numbers 3:42

wazaliwa wote wa kwanza

"wana wote wa kwanza"

Numbers 3:44

BWANA

Neno "BWANA" ni jina la Mungu ambalo alilitumia wakati alipojifunua kwa Musa kwenye kile kichaka kilichowaka moto. Jina "BWANA" linatokana na neno ambalo linamaanisha, "kuwa" au "kuwepo." Linaweza kumaanisha "Yeye ndiye" au "Mimi ndiye" au "Yeye anayewezesha vitu kuwepo". Jina hili linafunua ukweli wa Mungu kuwa alikuwepo na ataendelea kuwepo daima. Jina hili linaandikwa kwa herufi kubwa kubwa ili kulitofautisha na neno Bwana ili kuonyesha heshima.

Musa

Musa alikuwa nabiina kiongozi wa Waisraeli kwa zaidi yamiaka 40. WakatiMusa alipokuwa mtoto mchanga: wazazi wake walimweka kwenye kikapu kisha kumtupa kwenye majani ya Mto Naili ili kumficha ili Farao Mmisiri asimwone. Umbu lake Miriamu alimtazama pale. Maishsa ya Musa yalisalimika pale binti wa Farao alipomwona na umchukua kisha akampeleka ikulu kulelewa. Mungu alimchagua Musa kuwaokoa wana wa Israeli kutoka utumwani na kuwapeleka kwenye nchi ya ahadi. Baada ya Waisraeli kutoka Misri; wakati wakizungukazunguka jangwani,Mungu alimpatia Musa vidonge viwili vya mawe vilivyokuwa vimeandikwa amri kumi za Mungu. Karibu na mwisho wa maisha yake, Musa aliona ile nchi ya ahadi, lakini Mungu hakumruhusu kuingia pale kwa sababu alishindwa kutii.

Mlawi, Lawi

Lawi alikuwa mmoja wa wana kumi n a mbili wa Yakobo au Israeli. Neno "Mlawi" linamaanisha mtu ambaye anatoka kwenye ukoo wa Lawi. Walawi waliajibika kulitunza hekalu na kuendesha ibaada za kidini, ambazo zilijumuisha sadaka na dhabihu na maombi. Makuhani wote wa Kiyahudi walikuwa Walawi, waliokuwa wametokana na Lawi. Lakini si Walawi wote walikuwa makuhani. Makuhani wa Kilawi walikuwa wametengwa na kuwekwa wakfu kwa ajili ya kazi maalumu ya kumtumikia Mungu hekaluni. Kuna watu wawili pia waliojulikana kwa jina la "Lawi" wanaonekana kwenye ukoo wa Yesu katika injili ya Luka. Mwanafunzi wa Yesu aitwaye Mathayo pia aliitwa Lawi.

Israeli, Waisraeli, taifa la Israeli

Jina "Israeli" ni jina ambalo Mungu alimpatia Yakobo. Linamaanisha, "aliyemng'ang'ania Mungu. Wana wa uzao wa Yakobo walijulikna kama "Watu wa Israeli," "taifa la Israeli," au "Waisraeli"

Numbers 3:46

za wokovu kwa

Nomino ya "wokovu" lnaweza kutafsiriwa kwa tendo la "okoa." "Kuokoa"

wazaliwa wa kwanza wa Israeli

"wana wa kwanza wa Israeli"

shekeli tano

shekeli moja sawa na gramu 11. Kwa hiyoni sawa na gramu 55 za fedha

wanaozidi idadi ya Waisraeli

Hii inamaanisha kuwa kulikuwa na wazaliwa wa kwanza wa kiume zaidi ya 273 miongoni mwa makabila mengine ya Israeli zaidi ya idadi yao ya Walawi wa kiume.

Utazitumia hizo shekeli kwa kipimo cha mahali patakatifu

Hii inamaanisha kuwa shekeli itapimwa kwa kwa kipimo sawa na kile cha shekeli za mahali patakatifu. "Utatumia kipimo cha shekeli za mahali patakatifu"

gera ishirini

"gera 20."Gera ni kipimo kilicho sawa na kilogramu 0.57

kwa kipimo cha wokovu ulicholipa.

Hapa neno "bei" linamaanisha shekeli ambazo Musa alikuwa amekusanya, "zile pesa ambazo umekusanya kwa ajili ya wokovu"

Numbers 4

Numbers 4:1

Kohathi

Tazama 3:17

kati ya miaka thelathini na hamsini

"kati ya miaka 30 hadi 50"

wataungana na kundi

Neno "kundi"linamaanisha wale watu wengine wanaofanya kazi kwenye hema ya kukutania.

vilivyohifadhiwa kwa ajili yangu

"ambavyo nimevichagua kwa ajili yangu"

Numbers 4:5

Wakati kambi inajiandaa

Neno "kambi" linamaanisha watu wote waliokambini. "Wakati watu wanapojiandaa"

kusonga mbele

"kwenda kwenye eneo lingne"

kulifunika sanduku la ushuhuda kwa .. hilo

Kiwakilishi "hilo" kinamaanisha pazia ambalo lilitenganisha kati ya mahali patakatifu na patakatifu pa patakatifu.

watachomeka hiyo miti

"chomeka hiyo miti kwenye hizo peete pembeni za sanduku.

Numbers 4:7

mikate ya wonyesho

Mikate hii inawakilisha uwepo wa BWANA. "mikate ya uwepo wa BWANA"

Juu yake wataweka

Kiwakilishi cha "yake" kinamaanisha ile nguo ya rangi ya samawi.

sahani, vijiko, mabakuli ya kumiminia

"mabakuli navikombe vinavyotumka kwa kumiminia sadaka ya vinywaji"

Watavifunika

Neno "vi" inamaanisha yale masahani, vijiko, mabakuli na vikombe."

Mikate itakuwepo daima

"Lazima kuwepo na mikate daima"

kitambaa cha rangi nyekundu

"kitambaa chekundu"

kuweka miti ya kubebea

"kuweka miti kwenye pete pembezoni mwa meza"

Numbers 4:9

Wataweka ... vikiwa vimefunikwa na ngozi za pomboo"

"Lazima wavifunika ...na ngozi za pomboo"

Wataviweka kwenye miti ya kukibebea

"wataviweka vitu vyote hivi juu ya miti ya kubebea"

kuweka ile miti ya kubebea

"kuweka miti ya kubebea kwenye zile pete zilizo pembezoni mwa madhabahu"

Numbers 4:12

miti ya kubebea

Hiki ni chombo cha miti chenye umbo la mstatili kilicho na nguzo za kubebea vitu.

kwa kazi ya madhababahuni

"vinavyotumika wakati wa kutoa huduma ya BWANA mahali patakatifu"

katika kazi ya madhabahuni

"wakati wa kutoa huduma madhabahuni"

kuweka ile mitiy a kubebea

"Weka ile miti ya kubebea kwenye zile pete zilizo pembezoni mwa madhabahu"

Numbers 4:15

kubeba vitu vya mahali patakataifu

"kubeba vitu vyote vya mahali patakatifu"

kambi itakapoanza kuendelea mbele

"wakati watu watakapoende mbele"

Kohathi

TAzama 3:17

vyombo vitakatifu

"vifaa vitakatifu

mafuta ya taa

"mafuta kwa ajiliya taa"

atasimamia u,inzi

"wale wanaolinda"

Numbers 4:17

Wakohathi

Tazama 3:27

Kuondolewa kati ya Walawi

"kufanya chochote ambacho kitanifanya mimi kuwatoa kabisa miongoni mwa Walawi."

kwa kufanya hivi

Kirahi hiki kinalenga kitu ambacho BWANA atasma baadaye. Musa atawalinda Wakohathi kwa kutowaruhusukuingia ndani na kuona mahali patakatifu.

kazi maalumu ya kufanya, kila mmoja

virai hivi viwili vinamaanisha jambo lilelile na vimeunganishwa ili kutoa msisitizo.

Numbers 4:21

kwa wana wa Gerishoni

kwa wana wa kiume wa Gerishoni

Gerishoni

Tazama 3:17

kuanzia umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini

"kuanzia miaka 30 hadi miaka 50"

kuungana na wala wanaotumika katika hema ya kukutania

Tazama 4:1

Numbers 4:24

Hii ndiyo kazi ya koo za ... wanachotumikia na wanachobeba

Hi ni sentensi inayofafanua kile kinachoelezwa na mistari inayofuata.

Wagerishoni

Tazama 3:21

vifuniko vvya ngozi ya pomboo ambavyo vipo juu yake

"ni kifuniko cha nje kiinachotengenezwa kwa ngozi za pomboo"

Chochote kinachotakiwa kufanywa kutokana na vitu hivi

"kazi yeyote ambyo inahitajika kwa ajili ya kazi hii."

Numbers 4:27

watakaoongoza

"kusimamia"

Huu ndio utumishi wa Wagerishoni ... hema ya kukutania

Neno "utumishi" ni nomino zahania ambayo inaweza kuelezekakwa kutumia kitenzi. na neno hili linamaanisha kile ambacho BWANA alikuwa amesema. "Hii ndiyo namna ya utumishi wa wana wa ukoo wa kizazi cha Wagerishoni ambavyo watatumika katika hema ya kukutnia"

Ithamari

Tazama 3:1

Numbers 4:29

Uzao wa Merari

"uzao wa wana wa kiume wa Merari"

Merari

Tazama 3:17

uwapange

"uwaorodheshe"

umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini

"umri wa miaka 30 hadi umri wa miaka 50"

atakayeungana na kundi lenye utumishi katika hema ya kukutania

Tazama 4:1

Numbers 4:31

Huu ndio wajibu wao

"Huu" inamaanisha kile ambacho BWANA atasema baadaye.

mbao za masikani, mataruma, ... na vifaa vyake.

Kiwakilishi cha "zake" kinamaanisha nguzo za ua.

nguzo za ua zinazozunguka, nguzo, mbao ... na kamba zake

Tazama 4:31

Waoredhesha kwa majina na majukumu yao

"Uorodheshe kila jina la mtu na jukumu lake"

Numbers 4:33

chini ya uongozi wa Ithimari mwana wa Haruni kuhani mkuu

"Kama Ithimari nwana wa Haruni atkavyokuwa akiwaongoza"

Ithimari

Tazama 3:1

Numbers 4:34

Wana wa uzao wa Wakohathi

Hii inamaainsha wale wana wa kiume. "Wana wa wa kiume wa uzao w a Wakohathi"

Wakohathi

Tazama 3:27

Wenye umri wa miaka thelathini hadi umri wa wa miaka hamsini

"Miaka 30 umri wa miaka 50"

kila mmoja aliyepaswa kuungana na kundi

"kila mmoja aliyekuwa ameamriwa kuunagana na kundi"

kuungana na kundi linalotoa huduma y a utumishi kwenye hema ya kukutania

Tazama 4:1

2,750

"elfu mbili, mia saba na hamsini"

Numbers 4:38

Uzao wa Gerishoni

"Wana wa kiume wa uzao wa Gerishoni"

Uzao wa Gerishoni walihesabiwa

"Musa na Haruni waliwahesabi wana wa uzao wa Gerishoni

Kuanzia umri wa miaka thelathini hadi umri wa miaka hamsini

"kuanzia umri wa miaka 30 hadi umri wa miaka 50"

kwa kila mmoja anayetakiwa kuungana na kundi

Kila mmoja aliyetakiwa kuungana na kundi"

walihesabiwa kufuata koo zao

"ambao Musa na Hruni waliwahesabu kwa kufuata koo zao"

2,600

"wanaume 2600"

Numbers 4:41

walifanya hivi ili kutii

Kiwakilishi "wa" kinamwakilisha Musa na Haruni

Numbers 4:42

Uzao wa Merari walihesabiwa

"Musa na Haruni waliwahesabu uzao wa Merari"

Kuanzia umri wa miaka thelathini hadi umri wa miaka hamsini"

"kuanzia miaka 30 hadi miaka 50"

kila anayepaswa kuunga na na kundi

"kila mmoja aliyekuwa amepangiwa kuungana na kundi"

kuungana na watu wanotumika kwenye hema ya kukutania

tazama 4:1

waliohesabiwa kupitia koo zao

"ambao Musa na Haruni waliwahesabu kpitia koo zao"

Numbers 4:45

walitii

Kiwakilishi "wa" kinamwakilisha Musa na Haruni

Numbers 4:46

kuanzia thelathini hadi hamsini

Hii inamaanishsa wanaume. "wanaumekuanzia umri wa miaka thelathini hadi hamsini"

kuanzia thelathini hadi hamsini

Hii inamaanishsa wanaume. "wanaumekuanzia umri wa miaka thelathini hadi hamsini"

Numbers 4:49

Kwa agizo la BWANA

"Kama vile BWANA alivyoagiza"

na kutunza kumbukumbu ya kazi ambayo kila mmoja anaweza kufanya.alimwesabu kila mwanaume kwa jukumu alilofanya

Virai hivi viwili vinamaanishakitu kimoja na vimetumka pamoja ili kusisitiza jinsi Musa alivyowahesabu wanaume wote.

kile ambacho BWANA alikuwa amewaagiza kufanya

"kwa aina ya kazi ambayo alikuwa amemwagiza kila mmoja kufanya"

anaweza kufanya

"ambayo angekuwa nayo"

walitii ambacho BWANA alikuwa amewaagiza

kiwakilishi cha "wa" na "me" kinamlenga Musa na Haruni.

Numbers 5

Numbers 5:1

wenye magonjwa ya ngozi

Hii inamaanisha ukoma, huu ni ugonjwa unaoathiri ngozi na unasambaa kwa wengine kwa urahisi.

vidonda vinavyotoa harufu

Hii inamaanisha vidonda vya wazi vinavyotoa usaha.

ambaye amenajisika kwa kugusa maiti

Mtu alipogusa maiti alionekana kuwa najisi. Mtu ambaye alikuwa hakubariki kwa matumizi ya kazi ya Mungu alionekana ki mwili kuwa najisi.

umtoe kambini

kiwakilishi cha "u" ni cha wingi na kinamanisha watu wa Israeli.

Watu wa Israeli walifanya hivyo

Watu wa Israeli waliwatoa kambini watu waliokuwa najisi.

Numbers 5:5

dhambi yeyote ambayo watu hufanyiana

"dhambi yeyote ambayo watu hufanya dhidi ya mwingine"

mtu huyo atakuwa na hatia kwangu

"mtu huyo atakuwa amenikosea mimi pia"

malipo ya hatia yake

"kiwango sahihi cha fedha kwa dhambi yake"

na kuongeza kwenye malipo hayo sehemu ya tano zaidi

sehemu ya tano zaidi. Hii inamaanisha kuwa mtu atalipa sehemu ya tano zaidi ya malipo anayotakiwa kulipa.

sehemu ya tano

Sehemu ya tano ni sehemu moja kati ya vitu vitano.

Numbers 5:8

Lakini k ama mtu huyu aliyetendewa kosa hana ndugu wa kupokea hayo malipo

Lakini kama mtu aliyetendewa kosa amekufa na hana ndugu wa karibu wa kupokea malipo hayo"

kama mtu aliyetendewa kosa

"kama mtu ambaye mtu mwenye hatia amemtendea kosa"

basi atalipa hayo malipo ya hatia kwangu kupitia kwa kuhani.

kama mtu atalipa malipo hayo kwa kuhani kulipia hatia yake ni sawa na kulipa malipo hayo kwa BWANA.

kutoa fidia kwa ajili yake

"kutoa fidia kwa ajili ya dhambi yake"

vitu ambavyo vimetengwa na vikaletwa kwa kuhani na watu wa Israeli

"vitu ambavyo watu wa Israeli wamevitenga na kuvileta kwa kuhani"

sadaka ya kila mtu itakuwa ya kuhani; kama mtu yeyote atatoa kitu chochote kwa kuhani, kitakuwa chake

Virai hivi viwili vinamaanisha kitu kilekile na vinaweza kuunganishwa ili visomeke kuwa, 'sadaka ambayo mtu hutoa huwa mali ya kuhani ambaye wamepewa.

Numbers 5:11

kama mke wa mtu ataasi na kuafanya dhambi dhidi ya mume wake

Hiki ni kituambacho kinaweza kutokea, BWANA anamwambia Musa jinsi ya kufanya iwapo kama kitu hiki kitatokea.

Mke wa mtu ataasi

kama mke wa mtu si mwamiinifu

na kufanya dhdambi dhidi ya mume wake

"akafanya dhambi dhidi ya mume wake kwa kulala na mwanamume mwingine"

Numbers 5:13

Halafu mtu mwingine akalala naye

na mtu mwingine akalala naye

atakuwa amenajisika ... mke wake amenajisika ... mke wake hajanajisika

"amejinajisi mwenyewe ... mke wake amejinajisi mwenyewe ... mke wake hajajinajisi mwenyewe"

katika tendo

"katika tendo la uzinzi" au "kulala naye"

ile roho ya wifu itaendelea kumjulisha yule mume.

Hapa neno "roho" linamaanisha mtazamo na hisia za mtu. Wivu wake umeongolewa kama kuna mtu ambaye anamwambia, "Yule mtu anaweza kujihisi wivu na kuanza kumhofia"

roho ya wivu inaweza kumdanganya yule mwanamume

mwanamume anaweza kuwa na wivu bila sababu.

Numbers 5:15

sehemu ya kumi

hii ni sehemu moja kati ya kumi

sehemu ya kumi ya efa

sehemu ya kumi ya efa ni karibu sawa na lita 2.

ni sadaka ya unga ya wivu

"ni sadaka ya unga inayotolewa kwa ajili ya wivu"

dalili ya dhambi

"Dalili" ni kitu kinachoonyesha uhakika wa jambo fulani. kwa ahali hiyo alitoa sadaka inayoonyesha kama mke wake kweli alifanya uzinzi au la.

Numbers 5:16

karibu na kumweka mbele ya BWANA

"Katika uwepo wa BWANA." Kuhani atamleta karibu na madhabahu. "Karibu na madhabahu na kumweka karibu mbele za uwepo wa BWANA."

Numbers 5:18

mbeleza BWANA

"katika uwepo wa BWANA"

sadaka ya unga kwa ajili ya wivu

Tazama 5:15

kama hujafanya uzinzi

"kama haujaonyesha kutokuwa mwaminifu kwa mme wako"

na kufanya uovu

"kwa kufanya uovu maana yake ni kufanya uzinzi."

utakuwa huru na maji haya machungu

"haya maji machungu hayakuletea madhara"

haya maji machungu yanaweza kuleta laana

maji machungu yanaelezwa kama maji yanayoweza kuleta laana. Maana yake ni kwamba yule mwanamke atakapoyanywa maji haya yanaweza kumfanya asizae watoto,, hasa kama ana hatia.

Numbers 5:20

chini ya mume wako

"chini ya mamlaka ya mume wake"

umekengeuka

"hakuwa mwaminifu kwa mume wake"

umenajisika

"umejinajisi mwenyewe"

kinachoweza kuleta laana kwake

"ambacho kinaweza kusababisha laana kuja"

BWANA atakufanya wewe kuwa laana ... kuwa hivyo kwa watu wako

Kwa sababu BWANA anakulaani, watu wengine watakulaani pia, na BWANA atawaonyesha watu kuwa umelaaniwa kabisa"

itakayooneshwa kuwa hivyo kwa watu wako

"atakayoionesha kwa watu wako kuwa laana"

na kulifanya tumbo lako kuvimba na mapaja yako kuoza

Maana ya sentensi hii yaweza kuwa: 1) mwanamke hataweza kuzaa watoto. 2) mimba ya mwanamke itakooma mapema na yule mtoto atakufa.

mapaja yako kuoza

Neno mapaja, ni tafsida inayoonesha tumbo la mwanamke au sehemu zake za siri. "tumbo lako kuwa si kitu"

Numbers 5:23

na kisha kuzifuata laana zilizoandikwa

Hii inamaanisha kufuta wino ulio kwenye gombo

laana zilizoanadikwa

laana alizoziandika

Numbers 5:24

Taarifa kwa ujumla

Mpangilio wa matukio ulio kwenye hii mistari unachangaya sana, umeandikwa kwa mfumo huu ili kuonesha jinsi yale maji yawezavyo kuleta laana. Inaonekana kuwa mwanamke anapoyanywa yale maji; kuhani naye anateketeza ile sadaka, kisha yule mwanamke anayanywa yale maji tena. Anayanywa yale mara moja.

Naye kuhani atamwelekeza yule mwanamke kunywa yale maji ... yale maji yaletayo laana yataingia na kuwa machungu

Inaweza kusaidia kama mpangilio utatengenezwa upya kwa kuuweka mstari wa 24 unaoelezea habari ya mwanamke kunywa yale maji, baada ya mstari wa 26.

sadaka ya kuwakilisha

kiasi cha konzi ya unga kinawakilisha sadaka yote ya unga. Na maana yake halisi ni kwamba sadaka yote ni ya BWANA.

sadaka ya unga ya wivu

Tazama 5:15

Numbers 5:27

kama alinajisika kwa sababu alifanya uovu

"kama alikwa amejinajisi mwenyewe kwa sababu ya kufanya uovu"

alifanya uovu

"alifanya uzinzi"

Tumbo lake litavimba na paja lake litavimba

Tazama 5:20

Yule mwanamke atalaaniwa kati ya watu wake

"Watu wake watamlaani"

hajanajisika

"hajajinajisi mwenyewe"

na kama ni msafi

"hana hatia"

basi atakuwa huru

yaweza kumaanisha 1)"basi hatalaaniwa 2) "basi yuko huru katika hatia"

atabeba ujauzito

"atakuwa mjamzito"

Numbers 5:29

sheria ya wivu

"sheria inayoshughulikia maswala ya wivu"

anayekengeuka kwa mume wake

"ambaye si mwaminifu kwa mumewe"

na kunajisika

"na kujinajisi mwenyewe"

ile roho ya wivu

tazama 5:13

mwenye roho ya wivu kwa mkewe

"kumwonea wivu mke wake kuwa si mwaminifu kwake"

mbele ya BWANA

"katika uwepo wa BWANA"

Numbers 5:31

Atakuwa hana hatia ya kumleta mke wake kwa kuhani

"atakuwa hana hatia ya kufanya jambo lenye makosa kwa kumleta mke wake kwa kuhani"

atauchukua"

"atavumilia"

Numbers 6

Numbers 6:1

ataweka nadhiri ... kwa kuwa ni mnadhiri

"kuwa mnadhiri" maana yake ni kujiweka wakfu"

atajiepusha

Hii nahau inamaanisha kuwa mtu huyo lazima asinywe hivyo vinywaji wala chakula kilichokatazwa.

kilio kiinachotengenezwa na siki

"kileo ambacho watu hutengeneza kutokana na siki"

siki

ni kinywaji kinachotokana na divai ilichachushwa kwa muda mrefu na kuwa kinywaji kikali na kichungu

kilevi

"au siki iliyotengenezwa kutokana na divai kali"

zabibu zilizokauka

"zabibu zilizokaushwa"

ambazo amejitenga

"amejitenga kwa ajili yangu"

asile chochote kinachotokana na zabibu

"asile chochote ambacho watu huetengeneza kutokana na zabibu"

wala kitu chochote kitokanacho na makokwa hadi maganda

"kutokana na kitu chochote cha mizabibu"

Numbers 6:5

Nadhiri yake

Neno nadhiri humaanisha "kuwekwa wakfu"

wembe usipite kichwani mwake

"asipatikane mtu wa kutumia wembe juu ya kichwa chake"

siku za nadhiri yake kwa BWANA

Neno "nadhiri" ni "nomino zahania ambalo linweza kutumika kama kitenzi. Neno "nadhiri" hapa hapa linamaanisha kuwekwa wakfu. "siku ambazoamejiweka wakfu kwa BWANA"

kwa BWANA zitimilike

kwa BWANA zitimilike

Lazima ajitenge kwa BWANA

Lazima ajitenge mwenyewe kwa BWANA

Numbers 6:6

Kujidhiri ... amejitenga ...kujidhiri

Kujidhiri ni kujiweka wakfu.

Asijinajisi

Unajisi ni hali ya kutokukubalika kwa ajili ya matumizi ya BWANA.

ametengwa

amejitenga mwenyewe

wakati wa kujidhiri kwake

kwamba amejitenga mwenyewe

alijitunza kwa ajili ya BWANA

amejitunza kwa ajili ya BWANA.

Numbers 6:9

kukitia unajisi kichwa chake

Neno "kichwa"linamaanisha nywele za mnadhiri ambazo ni ishara ya kiapo chake. "amezinajisi nywele zake ambazo zinamwosha kila mtu kuwa kuwa amejitenga kwa ajili ya Mungu"

katika siku ya kujitakasa

"katika siku ambayo mwenyewe anajiweka kukubalika kwa Mungu"

siku ya saba

"siku YA 7"

Numbers 6:10

Siku ya nane

"Siku ya 8"

Numbers 6:12

katika siku hizo za utakaso

"katika siku hizo ambazo atawekwa wakfu"

Atalaetea kondoo mume kama ... sadaka ya hatia

"Ataleta kondoo mume wa mwaka mmoja kwa kuhani kuwa sadaka ya hatia"

Zile siku za kabla ya kunajisika hazitahesabiwa

"Hatazihesabu zile siku za kabla ya kunajisika"

kujiweka wakfu kwake kulinajisika

"alijifanya mwenyewe kutokukubalika kwa BWANA"

Numbers 6:13

muda wa kujidhiri kwake

"kujidhiri" kunamaanisha "kuwa wakfu". "kuwekwa kwake wakfu"

Ataletwa

"ataletwa na mtu"

Ataleta sadaka yake kwa BWANA

"ataleta sadaka yake kwa BWANA kupitia kwa kuhani ambaye ndiye ataitoa hiyo sadaka"

mikate iliyotengenezwa bila amira

"mikate iliyotengenezwa bila chachu"

unga mwembamba uliochanganywa na mafuta

"unga mwembamba aliouchanganya na mafuta"

mikate ya kaki isiyo na amira iliyopakwa mafuta,

mikate ya kaki isiyo na chachu ambayo aliipaka mafuta

mikate ya kai isiyo na amira

"vipande vidogovidogo vya mikate"

pamoja na sadaka za unga na sadaka za vinywaji

"pamoja na na sadaka za unga ambazo BWANA alitaka ziambatane na sadaka zingine.

Numbers 6:16

Atazitoa sadaka zake za dhambi

kiwakilishi "a" kinamaanisha kuhani. Na kiwakilishizake "zake" kinamlenga yule mtu anayetoa kiapo.

sadaka ya amani

"kuwa sadaka ya amani"

Pia kuhani atatoa ... sadaka ya vinywaji

"Pia kuhani atazitoa ... sadaka za vinywaji kwa BWANA"

Numbers 6:18

kama ishara ya kujitenga

"Ishara ya kuwa wakfu"

Numbers 6:19

bega la kondoo mume lililotokoswa

"lile bega la kondoo ambalo amelitakasa"

ishara ya kijidhiri

ishara ya kuwa wakfu" au "ishara inayoonyesha kuwa amaejiweka wakfu kwa BWANA"

Kisha kuhani atavitikisa

"kisha kuhani atavirudisha nyuma na kuvititsa"

pamoja na

"pia akiwa na"

cha kutikiswa

"ambacho kuhani alikitikisa"

lilitolewa

"ambalo alilitoa"

Numbers 6:21

kujidhiri kwake

"kujiweka kwake wakfu"

chochote atakachotoa

"kama ataamua kutoa sadaka yeyote ya nyongeza"

lazima atafanya kama alivyoapa

"Lazima aendelee kutii matakwa ya kiapo alichoaapa"

lazima atafanya kama alivyoapa ... kulinda ahadi yake kama ilivyoaanishwa katika sheria ya mnadhiri.

Virai hivi viwili kimsingi vina maana moja. Vimetumika kuonyesha msisitizo kuwa lazima atii sheria za kiapo.

kama ilivyoaanishwa katika sheria ya mnadhiri

"kama ahadi ya sheria ya mnadhiri inavyoainisha"

Numbers 6:22

Mtawabariki wana wa Israeli

kiwakilishi "m" ni cha wingi

BWANA na awabariki na kuwatunza

Kiwakilshi cha "wa" ni cha umoja

na kuwatunza

neno "kuwatunza" linamaanisha "kuwalinda"

Numbers 6:25

awaangazie nuru ya uso wake

Hii ninahau inayomanisha "BWANA atoe tabasamu lake"

awatazame kwa neema

"akuonyeshe neema"

BWANA awaangazie nuru ya uso wake ...na awape amani

Kiwakilishi cha "a" ni cha umoja

wanaweza kuwapa jina langu

"watawafanya watu wa Israeli wajue kuwa wao ni wangu"

Numbers 7

Numbers 7:1

Musa alikamilisha masikini

"Musa alikamilisha ujenzi wa masikani"

viongozi wa israeli na wale vichwa vya familia

"viongozi wa Israeli ambao pia ni vichwa vya familia za mababu zao"

vichwa vya familia za mababu zao

"viongozi wa familia za mababu zao"

WAlisaidia kuwahesabu watu kwenye ile sensa

"walimsaidia Haruni na Musa kuwahesabu wale wanaume"

Walileta sadaka zao kwa BWANA ... Walileta vitu hivi mbele za masikani.

"Walileta sadaka zao kwa BWANA wkazikabidhi kwake mbele ya masikani"

Wlileta magari sita yaliyofunikwa na mafahri kumi na sita

"magari sita na mafahari 12"

Numbers 7:4

kwa kila mmoja kadri ya uhitaji wa kazi yake

"kwa kila mwanamume kama alivyowahitaji kwa kazi yake"

Numbers 7:6

Gerishono ... Merari

Tazama 3:17

kwa sababu ndivyo kazi yao ilivyohitaji

"kwa sababu hivyo ndivyo walivyowataka wafanye kazi yao"

chini ya uangalizi wa Ithamari mwana wa Haruni kuhani

"chini ya usimamizi wa Kuhani Ithamari mwana Haruni" au "Ithamri mwana wa Haruni kuhani alisimamia kazi yao"

Ithamri

Tazama 3:1

Alifanya hivi kwa sababu

Kiwakilishi "a" kinamwakilishsa Musa

kwa sababu ya uhitaji wa kazi yao

"kwa sababu hivyo ndivyo walivyowataka wafanye kazi zao"

Numbers 7:9

hakuwapa chochote

Inamaanisha yale magari na wale mafahari

Kohathi

Tazama 3:17

wao waliangalia

"kazi yao ilikuwa"

vitu vitakatifu

"vitu ambavyo BWANA aliviweka kwa ajili ya masikani"

Numbers 7:10

walitoa bidhaa zao

"walitoa sadaka"

kila kiongozi alitoa sadaka kwa siku yake

"Kila siku, kiongozi mmoja alitoa sadaka yake"

Numbers 7:12

Siku ya kwanza

"siku ya 1"

Nashoni mwana wa Amiinadabu

Tazama 1:7

sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130

sahani moja ya fedha inayokaribiauzito wa kiligramu moa na nusu" au sahani moa ya fedha yenye uzani wa kiligramu moja na gramu 430"

bakuli moa yafedha ambayo uzito wake ni shekeli sabini

"bakuli moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 70" au "bakuli moja ya fedha yenye uzito wa garamu 770"

kwa kipimo cha mahali patakatifu

"iliyopimwa kwa kipimo kinachotumika mahali patakatifu"

unga mwembamba uliochanganywa na mafuta

"unga mwembamba ambao umechanganywa na mafuta"

bakuli moja la dhahbu lenye uzani wa shekeli kumi

"bakuli moja la dhahabu ambalo uzani wake ni gramu 110"

Numbers 7:15

wa mwaka mmoja

"ambao kila mmoja alikuwa na umri wa mwaka mmoja"

"Hii ilikuwa sadaka ya Nashoni mwana Aminadabu"

"Hii ndiyo Nashoni mwana wa Aminadabu aliyotoa"

Nashoni mwana wa Aminadabu

Tazama 1:7

Numbers 7:18

siku ya pili

"siku ya 2"

Nathanieli mwana wa Zuari

Tazzama 1:7

sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130

Tazama 7:12

bakuli moja ya fedha yenye uzani wa shekeli sabini

Tazama 7:12

kwa kipimo cha shekeli za mahali patakatifu

Tazama 7:12

unga mwembamba uliochanganywa na mafuta

"unga mwemba ambao aliuchanganya na mafuta"

Numbers 7:20

Bakuli moja la dhahabu lenye uzani wa shekeli kumi.

Tazama 7:12

wa umri wa mwaka mmoja

"ambao kila mmoja alikuwa na umri wa mwaka mmoja'

Hii ilikuwa sadaka y Nathanieli mwana wa Zuari

"Hii ndiyo Nathanieli mwana wa Zuari alichotoa"

Nathaniel mwana wa Zuari

Tazama 1:7

Numbers 7:24

sikuta tatu

"siku ya 3"

Eliabu mwana wa Heloni

Tazama 1:7

sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130

Tazama 7:12

bakuli moja la fedha lenye uza ni wa sheli sabini

Taza 7:12

kwa kipimo cha mahali patakatifu

Tazama 7:12

unga mwembamaba uliochanganywa na mafuta

Tazama 7:19

Numbers 7:27

wa mwaka mmoja

"ambao kila mmoja walikuwa na umri wa mwaka mmoja.

Hii ilikuwa sadaka ya Eliabu mwana wa Heloni

"Hii ndiyo sadaka ambayo Eliabu mwana wa Heloni alitoa"

Eliabu mwana wa Heloni

Tazama 1:7

Numbers 7:30

Siku ya nne

"siku ya 4"

Elizuri mwana wa Shedeuri

Tazama 1:4

Sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130

Tazama 7:12

Bakuli moja la fedha lenye uzani wa shekeli sabini

Tazama 7:12

Kwa kipimo cha mahali patakatifu

Tazama 7:12

unga mwembamba uliochanganywa na mafuta

Tazama 7:19

bakuli moja la dhahabu lenye uzani wa shekeli kumi

Tazama 7:12

Numbers 7:33

wa mwaka mmoja

"ambao kila mmoja walikuwa na umri wa mwaka mmoja.

Hii ndiyo iliyokuwa sadaka ya Elizuri mwana wa Shedeuri

"Hii ndiyo Elizuri mwana wa Shedeuri alichotoa kama sdaka"

Elizuri mwana wa Shedeuri

Tazama 1:4

Numbers 7:36

Siku ya tano

"Sikuy a 5"

Shelumieli mwana wa Zurishadai

Tazama 1:4

Sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130

Tazama 7:12

Bakuli moja la fedha lenye uzani wa shekeli sabini

Tazama 7:12

Kwa kipimo cha mahali patakatifu

Tazama 7:12

unga mwembamba uliochanganywa na mafuta

Tazama 7:19

Bakuli moja la dhahabu lenye uzani wa shekeli kumi

Tazama 7:12

Numbers 7:39

wa mwaka mmoja

"ambao kila mmoja alikuwa naumri wa mwaka mmoja"

Hii ndiyo sadaka ya Shelumieli mwana wa Zurishadai

"Hii ndiyo Shelumieli mwana wa Zurishadai alitoa kuwa sadaka"

Shelumieli mwana wa Zurishadai

Tazama 1:4

Numbers 7:42

siku ya sita

"siku ya 6"

Elisafu mwana wa Deuli

Tazama 1:12

sahani moja ya fedha yenye uzani shekeli 130

Tazama 7:12

bakuli moja la fedha lenye uzani wa shekeli sabini

Tazama 7:12

kwa kipimo cha mahali patakatifu

Tazama 7:12

unga mwembamba uliochanganywa na mafuta

Tazama 7:19

bakuli moja la dhahabu lenye uzani wa shekeli kumi

Tazama 7:12

Numbers 7:45

wa mwaka mmoja

"ambao kila mmoja alikuwa na umri wa mwaka mmoja"

Hii ndiyo Elisafu mwana wa Deuli alichotoa kuwa sadaka

"Hii ndiyo ambayo Elisafu mwana wa Deuli alitoa kuwa sadaka"

Elisafu mwana wa Deuli

Tazama 1:12

Numbers 7:48

siku ya saba

"siku ya 7"

Elishama mwana wa Amihudi

Tazama 1:10

Sahani moja ya edha yenye uzani wa shekeli 130

Tazama 7:12

bakuli moja la fedha lenye uzani wa shekeli sabini

Tazama 7:12

kwa kipimo cha mahali patakatifu

Tazama 7:12

unga mwembamba

Tazama 7:19

bakuli moja la dhahabu lenye uzani wa shekeli kumi

Tazama 7:12

Numbers 7:51

wa mwaka mmoja

"ambao walikuwa na umri wa mwaka wa mmoja kila mmoja"

Hii ndiyo iliopkuwa sadaka ya Elishama mwana wa Amihudi

"Hii ndiyo Elishama mwana wa Amihudi alichotoa"

Elishama mwana wa Amihudi

Tazama 1:10

Numbers 7:54

Siku ya nane

"siku ya 8"

Gamalieli mwana wa Pedazuri

Tazama 1:10

sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130

Tazama 7:130

bakuli moja la fedha lenye uzani wa shekeli sabini

Tazama 7:12

kwa kipimo cha mahali patakatifu

Tazama 7:12

unga mwembamba uliochanganywa na mafuta

Tazama 7:19

bakuli moja la dhahabu lenye uzani wa shekeli kumi

Tazama 7:12

Numbers 7:57

wa mwaka mmoja

"ambao kila mmoja alikuwa na umri wa mwaka mmoja"

Hiki ndicho Gamlieli mwana wa Pedazuri alitoa kuwa sadaka

"hiki ndicho Gamalieli mwana wa Pedazuri alitoa kuwa sadaka"

Gamalieli mwana wa Pedazuri

Tazama 1:10

Numbers 7:60

siku ya tisa

"siku ya 9"

Abidani mwana wa Gidioni

Tazama 1:10

sahani moja ya fdha yenye uzani wa shekeli 130

Tazama 7:12

bakuli mojala fedha lenye uzani wa shekeli sabini

Tazama 7:12

kwa kipimo cha mahali patakatifu

Tazama 7:12

unga mwembamba uliochanganywa na mafuta

Tazama 7:12

bakuli moja la dhahabu lenye uzani wa shekeli kumi

Tazama 7:12

Numbers 7:63

wa mwaka mmoja

"ambao kla mmoja alikuwa na umri wa mwaka mmoja"

"Hiki ndicho Abidani mwana wa Gidioini alitoa kuwa sadaka"

Hiki ndicho Aabidani mwana wa Gidioni alitoa kuwa sadaka"

Abidani mwana wa Gidioni

Tazama 1:10

Numbers 7:66

siku ya kumi

"siku ya 10"

Ahiezeri mwana wa Amishadai

Tazama 1:12

sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130

Tazama 7:12

bakuli moja la fedha lenye uzani wa shekeli sabini

Tazama 7:12

kwa kipimo cha mahali patakatifu

Tazama 7:12

unga mwembamba uliochanganywa na mafuta

Tazama 7:19

bakuli moja la dhahabu lenye uzani wa shekeli kumi

Tazama 7:12

Numbers 7:69

wa mwaka mmoja

"ambao kila mmoja alikuwa na umri wa mwaka mmoja"

Hii ndio ilikuwa sadaka ya Ahizeri mwana wa Amishadai

"Hiki ndicho Ahizeri mwana wa Amishadai alitoa kuwa sadaka"

Ahizeri mwana wa Amishadai

Tazama 1:12

Numbers 7:72

siku ya kumi na moja

"siku ya 11"

Pagieli mwana wa Okrani

Tazama 1:12

sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130

Tazama 7:12

bakuli moja la fedha lenye uzani wa shekeli sabini

Tazama 7:12

kwa kipimo cha mahali patakatifu

Tazama 7:12

unga mwembamba uliochanganywa na mafuata

Tazama 7:19

bakuli mojala dhahabu lenye uzani wa shekeli kumi

Tazama 7:12

Numbers 7:75

wa mwaka mmoja

wenye umri wa mwaka mmoja

Hii ndio sadaka ya Pagieli mwana wa Okrani

Hii ndiyo sadaka ambayo Pagieli mwana wa Okrani alitoa

Pagieli mwana wa Okrani

Tzama 1:12

Numbers 7:78

siku ya kumi na mbili

"siku ya 12"

Ahira mwana wa Enani

Tazama 1:12

sahani moja ya fedha yenye uzani wa shekeli 130

Tazama 7:12

bakuli moja la fedha lenye uzani wa shekeli sabini

Tazama 7:12

kwa kipimo cha mahali patakatifu

Tazma 7:12

unga mwembamba uliochanganywa na mafuta

Tazama 7:19

Bakuli moja la dhahabu lenye uzaniwa shekeli kumi

Tazama 7:12

Numbers 7:81

wa mwaka mmoja

Ambao kila mmoja alikuwa na umri wa mwaka mmoja

Hii ndio ilikuwa sadaka ya Ahira mwana wa Enani

"Hiki ndicho Ahira mwana wa Enani alitoa kuwa sadaka"

Ahira mwana Enani

Tazama 1:12

Numbers 7:84

walivitenga hivi vitu

kutenga ni kuweka wakfu. Maana yake ni kwamba sadaka hizi waliziweka wakfu kwa ajili ya BWANA

siku ambayo Musa alimimina mafuta kwenye madhabahu

neno "siku" linamaanishsa kipindi chote cha wakati huo. Viongoziwa Israeli waliviweka wakfu vitu hivi kwa muda wa siku 12. "Musa alipomimiina mafuta kwenye madhabahu"

kila sahani ya fedha ailikuwa na uzani wa shekeli 130.

Tazama 7:12

kila bakuli lilikuwa nanuzani wa shekeli 70

Tazama 7:12

kwa kipimo cha mahali patakatifu

Tazama 7:12

vyombo vyote vya fedha vilikuwa na uzani wa ... vyombo vyote vya dhahabu vilikuwa na uzani wa

"vyombo vyote vya fedha kwa pamoja... vyombo vyote vya dhahabu kwa pamoja vilikuwa na uzani wa"

vyombo vya fedha

Hii inamaanisha sadaka zote zile zilizokuwa zimetengenezwa kwa fedha, sahanizote na mabakuli.

Kila yale mabakuli kumi na mbili vya dhahabu... yalikuwa na uzani wa shekeli kumi

Tazama 7:12

Numbers 7:87

kumi na mbili ... ishirini na nne ... sitini

"12 ... 24 ... 60"

wa mwaka mmoja

"walikuwa na umri wa mwaka mmoja"

baada ya kumiminiwa mafuta

"Baada ya Musa kuimiminia mafuta"

Numbers 7:89

aliisikia sauti yake ikimwambia

"sauti yake" inamaanisha sauati ya BWANA. "alimsikia BWANA akimwambia"

kutoka juu ya kiti cha rehema ... kutoka kati kati ya makerubi.

Virai hivi viwili vinafafanua eneo moja

sanduku la ushahidi

Tazama 4:5

Alinena naye

"BWANA alinena na Musa"

Numbers 8

Numbers 8:1

lazima zimulike mbele

"lazima ziing'ae kuelekea mbele"

Numbers 8:3

ili ziangaze

"kuangaza"

kinara kilitengenezwa

"walikuwa wametengeneza kinara"

kutengenezwa kwa vikombe na kwa maua hadi juu

"kwa vikombe vilivyofuliwa vinavyofanana na maua"

Numbers 8:7

ili kuwatakasa

kiwakilishi "wa" kinawawakilisha Walawi.

uwanyunyizie maji ya takaso juu yao

"uwanyunyizie maji yanayoashiria utakaso"

wafue nguo zao

"waambie wafue nguo zao"

fahari mchanga na sadaka ya unga

Wakati wa kutoa sadaka ya fahari mchanga, sadaka ya unga ilitakiwa kuambatana nayo.

ya unga mwembamba uliochanganywa na mafuta

"ya unga mwembamba ambao wameuchanganya na mafuta"

Numbers 8:9

uwakusanye jamii yote

"wakusanye jamii yote"

mbele yangu, BWANA

BWANA imetumika kwa jina lake Mungu

Wana wa Israeli wataweka mikono yao juu ya Walawi

"Watu wa Israeli wataweka mikono yao juu ya Walawi, wakiwaweka wakfu kwangu"

kuwa sadaka ya kutikiswa

Haruni alitakiwa kuwatoa Walawi kwa BWANA kwa kiwango sawa cha kuwaweka wakfu kama ilivyo sadaka inayotolewa kwa BWANA. "kama ilivyo sadaka ya kutikiswa"

Numbers 8:12

Walawi wataweka mikono yao juu ya hao fahari

Hiki ni kitendo cha ishara kiniachowatambulisha Walawi kuwa sawa na wanyama wanaotolewa sadaka. Kwa namna hii mtu anajitoa mwenyewe kwa BWANA kupitia wanyama.

uwainue kuwa sadaka ya kutikiswa kwa ajili yangu

"uwaweke wakfu kwangu, kama vile unavyoinua sadaka ya kutikiswa"

Numbers 8:14

Uwatakase. Uwatoe kuwasadaka ya kutikiswa

"Lakini uwatakase kwanza, utawatakasa. utawatoa kama sadaka ya kutikiswa"

Utawatoa kuwa sadaka ya kutikiswa

"Utawaweka wakfu kwangu kuwa sadaka ya kutikiswa,kama vile unavyofanya wakati wa kutoa sadaka ya kutikiswa"

Numbers 8:16

kila mzaliwa wa kwanza afunguaye tumbo, mzaliwa wa kwanza.

Virai hivi viwili vinamaanisha jamabo lilelile ili kutoa msisitizo wa mzaliwa wa kwanza.

mtoto wa kiume afunguaye tumbo

"mtoto wa kiume ambaye ni mzaliwa wa kwanza kwa mama"

nilipowachukua

Hii ni tafsida inayotumika kuonyesha kitendo cha mtu anapomwua mtu. "Nilipomwua"

Niliwatenga

Kiwakilishi "wa" kinawawakilisha wazaliwa wa kwanza wa Israeli."

Numbers 8:18

Nimewatoa Walawi kuwa zawadi kwa Haruni na wanawe

Kitendo cha BWANA chca kuwatoa Walawi ili kumsaidia Haruni kinachukuliwa kuwa sawa na kuwa zawadi kwake ambayo BWANA aliitoa kwa Haruni na kwa wanae

Nimewachukua ... Nimewatoa

Kiwakilishi cha "wa" kinamaanishsa Walawi.

badala ya wazaliwa wa kwanza

"badala ya kuchukua wazaliwa wa kwanza"

wanapokaribia

"kiwakilishi cha "wa" kinawakilishsa wana wa Israeli.

Numbers 8:20

Musa, Haruni, na jamii ya Waisraeli wote ... waliwafanya Walawi hivi

"Musa, Haruni na watu wote wa Israeli waliwafanya Walawi kila kitu ambacho BWANA alikuwa amemwagiza Musa kuhusiana na Walaawi"

Numbers 8:22

kufanya utumishi wao

Neno "huduma" ni nomino zahania amabyo inaweza kutumika kama kitenzi "kuhudumia"

mbele ya Haruni na mbele ya wanawe

"katika uwepo wa Haruni na wanawe"

Kama BWANA

"Kile walichofanya kilikuwa"

Waliwahudumia Walawi wote kwa jinsi hii

"Waliwafanyia Walawi kile ambacho BWANA alikuwa amewaamuru. "Kiwakilishi cha "wa" kinamaanisha watu wa Israeli.

Numbers 8:23

Haya yote ni kwa ajili ya Walawi

"Amri zote hizi ni kwa ajili ya Walawi"

umri wa miaka ishirini na mitano

"miaka 25"

Wataungana wa wale wanaohudumia kwenye hema ya kukutania

Tazama 4:1

Numbers 8:25

Watakapokuwa na umri wa miaka hamsini

"katika umri wa miaka 50"

Numbers 9

Numbers 9:1

mwezi wa kwanza

"katika mwezi wa. 1" Huu ni mweziwa kwanza wa Kalenda ya Kihebrania. Inaanzia pale Mungu alipowatoa Wana wa Israeli kutoka Misri

mwaka wa pili

"mwaka wa 2"

baada ya kutoka katika nchi ya Misri

Kirai cha "kutoka katika" kinamaanisha kuondoka. "Baada ya kuondoka katika nchi ya Misri"

Wana wa Israeli ... katika wakati wake

Neno "wakati wake" linamaanisha wakati uliopangwa "muda wa nyuma". Hii inamaanisha watakapokuwa wakiimbuka kila mwaka.

Siku ya kum na nne ... kwa muda uliopangwa

Huu ni wakati wa uliopangwa kwa mwaka ili waisherehekeePasaka. "katika siku ya kumi na nne ... wataikumbuka, kwa kuwa huu ndio muda wa kuisherehekea kwa kila mwaka"

siku ya kumi na nne

"siku ya 14"

fuata sheria zake zote na ufuate taratibu zake zote

Virai hivi viwili vinamaanisha kitu kimoja, Vimetumika kuonyesha msisitizo wa kuzitii amri.

utaikumbuka

neno "ku" itunza" ni nahau inayomaanisha kuikumbuka. "mtaikumbuka" au "mtaisherehekea"

Numbers 9:4

wataishika sikukuu ya Pasaka

Neno "wataishika" linamaanisha kuikumbuka. "kuikumbuka sikukuu ya Pasaka" au "Kuisherehekea sikukuu ya Pasaka"'

katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza

"katika siku ya 14 ya mwezi wa 1"

Numbers 9:6

walionajisika kwa sababu ya maiti

"walinajisika kwa sababu ya kugusa maiti"

kunajisika

Mtu ambaye Mungu anamwona hakubaliki kiroho ni yule ambaye katika hali ya mwili alikuwa amenajisika.

kuishika Pasaka

Tazama 9:4

kwa sababu ya maiti

"kwa sababu tumegusa maiti"

kwa nini basi unatutaka tuendelee kutoa sadaka ... wana wa Israeli?

Si sahihi kutuzuia kutoa sadaka ... kati ya wana wa Israeli.

uliopangwa

"ulioamriwa"

Numbers 9:9

amenajisika

Tazama 9:7

kwa sababu ya maiti

"kwa sababu umegusa maiti"

Kuishika Pasaka

Tazama 9:4

Numbers 9:11

Watishika Pasaka

Tazama 9:4

Sikuy a kumi na nne ya mwezi wa pili

"siku ya 14 ya mwezi wa 2"

wa jioni

"wakati wa jua kuzama"

Wataila

"Watamla mwanakondoo wa Pasaka"

kwa mikate isiyotiwa chachu

"kwa mikate iliyotengenezwa bila amira" au "kwa mikate ambayo haina amira"

mboga chungu

hii ni mimea midogo midogo ambayo ina radha mbaya

kuvuunja mifupa yake

"wasivunje mifupa yake yeyote"

Numbers 9:13

mtu yeyote asiye najisi

Mtu ambaye anakubalika kwa Mungu kiroho ni yule ambaye anaonekana kuwa kimwili ni msafi

kuishika Pasaka

Tazama 9:4

huyo mtu lazima aondolewe

Neno "kuondolewa" linamaanisha kukatiliwa mbali.

uliopangwa

ulioamriwa

Huyo mtu lazima abebe dhambi yake

"Mtuhuyo lazima abebe adhabu ya dhambi yake"

anayeishi kati yenu

kiwakilishi cha "yenu" kinamaanisha watu wa Israeli

ataishika na kufuata amri zote

"huyo mgeni ataishika na kufuata yote ambayo BWANA ameamuru"

ataishika na kufuata amri zote , na kufuata taratibu zake

Virai hivi viwili vinamaanisha jambo lilelile, vimetumika kutia msisitzo wa kwamba huyo mgeni atazitii sheria zote na kuishika Pasaka.

katika nchi

"katika nchi ya Israeli"

Numbers 9:15

masikani iliposimamishwa

"Walawi walipoisimamisha ile masikani"

ile hema ya amri ya agano

Tazama 1:50

Lilionekana kama moto mpaka asubuhi

"Wakati wa usiku lile wingu lilionekana kama moto mkubwa mpaka asubuhi"

Liliendelea hivyo hivyo

"Lile wingu lilibaki hivyohivyo juu ya masikani"

na kuonekana kama moto wakati wa usiku

"lilionekana kama moto mkubwa wakati wa usiku."

Na kila wingu lilipochukuliwa

"lilipoondolewa" au "BWANA alipoliondoa wingu"

wingu liliposimama

"Wingu liliposimama kuendelea"

Numbers 9:18

kwa amri ya BWANA

"BWANA alipotoa amri"

Numbers 9:20

kwenye masikani

"juu ya masikani

waliweka kambi

"walipoweka kambi yao"

kuanzia jioni mpaka asubuhi

"kuanzia jioni mpakasubuhi tu"

kama liliendelea

"kama wingu lilibaki juu ya masikani"

ni pale tu wingu liliponyanyuliwa ndipo waliendelea

"kisha baada ya wingu kuondolewa ndipo waliposafiri"

Numbers 9:22

pale wingu liliponyanyuliwa

"BWANA alipolinyanyua wingu"

kwa amri ya BWANA

"kile ambacho BWANA alikuwa ameamuru"

amri ya BWANA ilyotolewa kupitia kwa Musa

amari ambazo BWANA alikuwa ametoa kupitia kwa Musa

Numbers 10

Numbers 10:1

tengeneza tarumbeta mbili za fedha

"mwambie mtu mmoja atengeneze tarumbeta mbili za fedha"

utazitumia hizo tarumbeta

Siye Musa atakayepiga hizo tatrumbeta bali atawaagiz amakuhani kuzipiga.

Numbers 10:3

mbele yako

"wakati ukiwepo." Yaani Musa akiwepo wakati Makuhani watakapozipiga hizo taraumbeta.

basi viongozi, vichwa vya koo za za Israeli

virai hivi viwili vinamaanishsa kitu kilekile. Kirai cha pili kinatumika kufafanua kirai cha kwanza. "Viongozi ambao ni vichwa vya koo za za Israeli"

Utakapopiga tarumbeta ya sauti kuu

"utakapopiga ishara kuu"

Numbers 10:6

utakapopiga tarumbeta kwa ishara kuu

"watakapopiga ishara kuu"

watu wote watakapokutana

"kuwakusanya watu pamoja"

mara ya pili

"mara ya 2"

watapiga tarumeta kwa sauti kuu ili kuanza safari

"kiwakilishi cha "wa" kinawawakilisha makuhani wa Israeli.

huu ndio utakuwa utaratibu wa watu

"utakuwa utaratibu wenu." "wenu" ni kiwakilishi cha wengi kinachomaanisha Waisraeli.

Numbers 10:9

Nanyi mtakapoenda vitani ... wanaowakandamiza

"Waisraeli wanapokuwa vitani ... kwa wale wanaowakandamiza Waisraeli"

ndipo mtakapotoa sauti ya ishara ya tarumbeta

"basi utawaamuru makuhani kupiga sauati ya tarumbeta "

nitawaita na kuwakumbuka

Kirai cha " kuwaita" kinamanisha kuwakumbuka. "Nitawakumbuka"

Numbers 10:10

wa kusherehekea

"mtakaposherehekea"

mtapiga tarumbet zenu

"utawaamuru makuhani kupigahizo tarumbeta"

katika miandamo ya miezi

Kalenda ya Kihebrania ina miezi kumi na mbili. wakatiwa mwezi kuanza ukiwa na ule mwanga rangi ya fedha unaonyesha mwanzo wa wa mwezi katika kalenda ya Kihebrania.

sadaka zenu za kuteketezwa na kwa sadaka zenu za amani ... kwangu

kiwakilishi "zenu" ni cha wingi kikimaanisha Waisraeli.

kwa heshima ya sadaka zenu

""kwa heshima ya sadaka"

Huu utakuwa ukumbusho wenu kwangu."

Hii itakuwa kumbukumbu yanagu kwenu". au "daima itanikumbusha."

Huu utakuwa

Neno "huu" linamaanisha zile tarumbeta na zile sadaka.

Numbers 10:11

mwaka wa pili

"katika mwaka wa 2." Huu ni mwaka wa pili baada ya BWANA kuwatoa Waisraeli kutoka nchi ya Misri.

Katika siku ya ishirini, mwezi wa pili.

"katika siku ya 20, ya mwezi wa 2." Huu ni mwezi wa pili wa Kalenda ya Kihebrania.

wingu liliinuliwa

"BWANA aliliinua wingu"

masikani ya amri za maagano

Tazama 1:50

amri ya BWANA ilitolewa kupitia kwa Musa

"amri ambayo BWANA aliamuru kupitia kwa Musa"

Numbers 10:14

Kambi ya mahali pa uzao wa Yuda

Kambi hii inajumuisha makabila matatu chini ya kikosi cha Yuda: Yuda, Isakari na Zabuloni.

iliondoka ya kwanza

"iliondoka ya 1". Kirai cha w"aliondoka" kinamaanisha walifungasha vitu vya kambi yao na kuanza safari.

Nashoni mwana wa Aminadabu

Tazama 1:7

Nathanaeli mwana wa Zuari

Tazama 1:7

Eliabu mwana wa Heloni

Tazama 1:7

Numbers 10:17

Gerishoni ... Merari

Tazama 3:17

jeshi la mahali pa kambi ya Reubeni

Hii inamaanisha majeshi ya kabila yaliyo chini ya kikosi cha Reubeni: Yaani Reubeni, Simioni, na Gadi.

Elizuri m wana wa Shedeuri

Tazama 1:4

Shelumieli mwana wa Zurishadai

Tazama 1:4

Elisafu

Tazama 1:4

Numbers 10:21

Wakohathi

Tazama 3:27

Majeshi ya kabila la uzao wa Efraimu

Haya ni majeshi yaliyokuwa chini ya kikosi cha Efaimu: Efraimu, Manase, na Benyamini.

Elishama mwana wa Amihudi

Tazama 1:10

Gamalieli mwana wa Pedazuri

Tazama 1:10

Abidani mwana wa Gidioni

Tazama 1:10

Numbers 10:25

Jeshi lililoweka kambi mahali pa bango la Uzao wa Dani

Hii k ambi ilikjumuisha kabila la Dani ambalo ni: Dani, Asheri, na Naftali.

Ahizeri mwana wa Aminadamu

Tazma 1:12

Pagieli mwana wa Okrani

Tazama 1:12

Ahira mwana wa Enani

Tazama 1:12

Numbers 10:29

Hobibu mwana wa Reuli

Hili ni jina la mwanamume

ambalo BWANA ametuahidi

"ambalo BWANA ametuahidi sisi"

tutawatendea mema

"tutawakarimu vizuri"

Numbers 10:31

Tafadhali msituache

"mtatuongoza na kutonyesha jinsi ya kuishi jangwani"

Numbers 10:33

Walisafiri

"kiwakilishi cha "wa" kinamaanisha Waisraeli

mlima wa BWANA

Huu ni mlima Sinai. "Mlima Sinai ni mlima wa BWANA"

Sandukula agano la BWANA liliwatangulia

"wale wanaume walilibeba sanduku la agano la BWANA mbele yao wakatiwote waliposafiri"

muda wote wa mchana

"kila mchana" au "wakati wa mchana"

Numbers 10:35

Kila hilo sanduku liliposafiri

"Kila wakati wale watu waliokuwa wamebeba sanduku walipoondoka"

Inuka BWANA

Kirai cha "inuka" ni ombi la BWANA kumtaka atende. Kwa hiyo Musa anamwomba BWANA awasambaze maadui wake.

Uwafanye wale wanaokuchukia kukukimbia

"uwafanye wale wanokuchukia kukimbia mbele ya sanduku lako na mbele ya watu wako"

na kila lile sanduku liliposimama

"kila watu wanobeba lile sanduku waliposimama"

hawa Waisraeli makumi elfu

Hii inamaanisha watu." hawa walio makumi elfu"

Numbers 11

Numbers 11:1

Moto kutoka kwa BWANA ukawaka

"BWANA alituma moto uliowaka"

Mahali pale paliitwa

"wakapaita mahali pale"

Numbers 11:4

Ni nani atakayetupatia nyama za kula?

"Tunatamani kama tungepata nyama tule"

na sasa hatuna hamuya kula

"hatutaki kula" au "hatuwezi kula"

Numbers 11:7

punje ya mtama

mbegu hii hutumika kama kiungo inapokuwa imekauka

bedola

hii ni kitu chenye rangi inayofanana na kijivu

Numbers 11:9

macho ya Musa

"katika fikra za Musa"

Numbers 11:11

Taarifa kwa ujumla

Musa anamlalamikia BWANA akitumia maswali mengi yasitotaka majibu.

Kwa nini umemtendea mtumishi wako vibaya namna? kwa nini hujapendezwa na mimi?

"usinitendee mimi, mtumishi wako, vibaya namna hiyo." au "usiwe na hasira dhidi yangu."

Umenifanya kubeba mizigo ya hawa watu

"umenifanya niajibike kwa ajili ya hawa watu"

Je, mimi ndiye niliyewatungia mimba hawa watu? Mimi ndiye niliyewazaa kiasi kwamba unaniambia?

"Mimi si baba wa hawa watu. Kwa hiyo si sahihi kuniambia mimi."

wabebe kwa ukaribu vifufani mwako kama baba abebavyo mtoto wake

Maana yake ni kwamba Musa analazimika kuajibika kwa watu ambao hawawezi kujilinda wenyewe, kama vile mzazi alindavyo kichanga.

Je, nitawabeba mpaka kwenye nchi ... mababu zao kuwapa?

""Usinitegeme mimi kuwabeba... mpaka kwenye uliyowaahidi mababu zao kuwapa" au "siwezi kuwabeba... mpaka kwenye nchi uliyowaahidi mababu zao."

Numbers 11:13

Naweza kupata wapi nyama za kuwapa watu wote hawa?

"siwezi kupata uwezekenio wa kupata nyama za kuwapatia watu wote hawa."

Mimi pekee yangu siwezi kuwabeba watu wote hawa

"Siwezi kuwapatia mahitaji yao watu wote hawa."

Ni wengi sana kwangu

"Wajibu huu ni mzito sana kwanagu"

Numbers 11:16

Sehemu ya roho iliyo ndani kwako

Neno "roho" linamaanisha mamlaka ambayo Roho wa Mungu alikuwa amempatia Musa ili kwamba Musa aweze kufanya yale amabyo Mungu alikuwa amemwamuru. "baadhi ya mamlaka ambayo Roho amekupatia wewe"

Nao watabeba mzigo wa watu pamoja na wewe

"Watakusaidia kuwaangalia watu hawa"

Na hautaubeba pekee yako

"Hautawaangalia pekee yako"

Numbers 11:18

Taarifa kw aujumla

BWANA anaendelea kuongea a Musa

nani atakayetupa nyama tule?

"Tunatamani kama tungepata nyama tule"

mpaka zitakapowatokea puani

Inaweza kumaanisha 1) Mungu anamaanishsa kutapika kupitia puani au mpaka mtaugua na kutapika 2)watakula nyama nyingi sana kama itakavyokuwa pale zitakapowatokea puani. au "mpaka mtaanza kujisikia kuwa zinataka kutokea puani"

kwa nini tulitoka Misri?

"Bora tusingelitoka Misri."

Numbers 11:21

Je, tutayachinja haya makundi ya ng'ombe na kondoo ili kuyatosheleza? Je tutawakamaata hawa samamki wote wa baharini ili kuwatosheleza?

"Tutatakiwa kuwachinja makundi yote ya ng'ombe na kuwakama samaki wote wa baharini ili kuwatosheleza!"

Ng'ombe na makundi

Maneno haya yanamaanisha kitu kimoja. Yametumika kuonyesha msisitizo wa kundi kubwa la wanyama

Smamki wote wa baharini

Musa ametumia mfano huu ili kuonyesha kuwa ilivyokuwa vigumu kuwapatia chakula watu wa Israeli.

ilikuwatosheleza

"kuwatosheleza njaa yao"

Je, mkono wangu ni mfupi?

"Je, mnadhani kuwa sina uwezowa kuyafanya haya?" au "manapaswa kujua kuwa mimi nina uwezo zaidi wa kuyafanya haya."

Numbers 11:24

Maneno ya BWANA

"Kile ambacho BWANA amesema"

Sehemu ya Roho aliyekuwa kwa Musa

Tazama 11:16

na kuiweka kwa wale wazee sabini

Tazama 11:16

Roho alipowashukia

"Walipokuwa na nguvu kutoka kwa Roho"

Numbers 11:26

Roho aliwashukia pia

"Roho alipa nguvu pia"

Majina yao yalikuwa yameandikwa kwenye orodha

"Musa alikuwa ameandika majina yao kwenye orodha"

Numbers 11:28

wazuie

"waambie waache kutoa unabii"

una wivu kwa niaba yangu

"unapaswa kutokuwa na wivu"

una wivu kwa niaba yangu

"Unadhani kuwa wanaweza kuwa wanacchukua kitu kutoka kwangu?"

angeweka Roho yake juu yao

"Kwsamba Roo ya BWANA angewapatia uwezo."

Numbers 11:31

kware

ndege mdogo

kiasi cha umabli wa safari ya siku moja upande huu na umbali wa siku moja upande mwingine

"ni umbali wa siku moja ambao mtu anaweza kwenda katika uelekeo wowotde.

kiasi cha mita moja toka uso wa dunia

"kiasi cha sentimita 92" au "mita moja"

hakuna aliyekusanya pungufu ya mita mbili

"kila mmoja alikusanya si chini ya mita mbili za ujazo"

mita mbii za ujazo

mita moja ya ujazo ni saw na lita 220."lita 2,200"

Numbers 11:33

wakati ile nyama ikiwa bado iko kwenye meno, wakiwa bado wanatafuna

Sentensi hizi zinamaanishakitu kimoja. "wakati walipokuwa bado wanakula ile nyama"

Mahali pale paliitwa Kibroti Hataava

"walipaita mahali pale Kibroti Hataava"

Hazeroti

Hili ni eneo la mahali fulani jangwani

Numbers 12

Numbers 12:1

Hivi BWANA amesema na Musa tu? Ni kweli hajawahi kusema nasi pia?

"BWANA hajasema na Musa tu. Pia amesema na sisi."

sasa BWANA akasikia

Neno "sasa" linavuta usikivu kwa kile ambacho kinafuata baadaye.

Sasa Musa alikuwa mtu

"Neno "sasa" limetumika kuonyesha mwanzo wa habari kuu. Msimuliaji anaeleza historia ya Musa kuhusu tabia zake.

Numbers 12:4

nguzo ya wingu

umbo la wingu linaongolewa kama vile ni nguzo. "wingu lenye umbo kama nguzo" au "wingu refu"

Numbers 12:6

Lakini si hivyo kwa mtumishi wangu Musa

"Siongei na Musa kwa namna hiyo"

Yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu

Nyumba hapa inamaanisha taifa la Israeli. Musa amawaongoza watu wangu kwa uamiinifu" au Musa ndiye ninayemwamini kuwaongoza watu wangu Usraeli"

Kwa nini hamuogopi kumnenea kinyume mtumishi wangu Musa?

"Mnapaswa kuogopa kumnenea kinyume mtumishi wangu, dhidi ya Musa"

kinyume, cha mtumishi wangu Musa

kinyume cha mtumishi wangu, Musa

Numbers 12:9

Hasira ya BWANA ikawawakia

Hasira ya BWANA inafananishwa na moto."BWANA akawakasirikia sana"

"akawa mweupe kama ukokoma"

"akawa mweupe sana"

Numbers 12:11

usituadhibu kwa sababu ya uovu wetu huu

Hii inamaanisha usituadhibu kwa sababu ya dhambi zetu

Tafadhali usimwache akawa kama mtoto mchanga aliyekufa amabye nusu ya nyama yake imeoza

"Tafadhali usimwache akawa kama mtoto mchanga ambaye nusu ya nyamya yake imeoza"

Numbers 12:13

Mungu ninakusihi umponye tafadhali

neno "tafadhali" limerudiwa ili kuonyesha msisitizo

kama baba yake angemtemea usoni

kumtemetemea mtu usoni ilikuwa udhi baya

Miriamu akafungiwa nje ya kambi

"Miriamu alitengwa nje ya kambi"

Miriamu akafungiwa nje ya kambi

"Musa alimfungia Miriamu nje ya kambi"

Numbers 12:16

Hazeroti

Tazama 11:13

Numbers 13

Numbers 13:1

ambayo nimewapa

"ambayo nimeamua kuwapeni

Kila mwanamume awe kiongozi katika kabila lake

"Kila mwanamume ambaye ulimtuma lazima awe kiongozi miongoni mwa kabila yake"

Numbers 13:3

Shamua mwana wa Zakuri

Haya ni majiina ya wanaume

Numbers 13:5

Shafati ... Hori ... Yefune ... Igali ... Yusufu ... Nuni

Haya ni majina ya wanaume

Numbers 13:9

Paliti ... Rafu ... Gadieli ... Sodi ... Gadi ... Susi ... Amieli ... Gemali

Haya ni majina ya wanaume

Kutoka kabila la Yusufu (Hiyo inamaanisha kutoka kabila la Manase)

Kutoka kwenye kabila la Mananse mwana wa Yusufu.

Numbers 13:13

Setu ... Mikaili ...Nabi ... Vofsi ... Geuli ... Machi

Haya yote ni majina ya wanaume

Hoshea mwana wa Nuni

Tazama 13:5

Numbers 13:17

Ni nzuri au mbaya? Miji yao ikoje iko kama kambi au ni miji yeneye ngome?

"Mkaone kama nchi ni nzuri au mbaya. ni aina gani ya miji iliyoko huko, na kama miji hiyo ni kama kambi au imezungushiwa ngome za ulinzi"

Je, iko kama kambi au ni miji yenye ngome

Miji yenye ngome ilikuwa na kuta imara zinazozunguka ili kuwalinda na majeshi ya maadui. Kambi hazikuwa na kuta za namna hii.

Numbers 13:21

Sini ... Rehobi ... Zoani

Haya ni majina ya maeneo

jangwa la Sini

Neno "Sini" ni jina la Kihebrania lenye maana ya jangwa.

Hebroni ilikuwa imejengwa miaka saba kabla ya Zoani ya Misri

"Wakanaani walikuwa wameijenga Hebroni miaka 7 kabla ya kuijenga Zoani"

Ahimani ... Sheshai ... Talmai

Haya ni majinia ya koo zilizokuwa zimeitwa kufuata mababu zao.

Anaki

Hili ni jina la mwanamume

Numbers 13:23

Eshikoli

Hili ni jina la mahali

Na makundi mawili ya wapelelezi

"kati ya watu wawili wa makundi hayo"

Mhali pale paliitwa

"walipaita mahali pale"

Numbers 13:25

Baada ya siku arobaini

"Baada ya siku 40"

Wakaleta taarifa kwao

"wakaleta taarifa" au "wakaleta taarifa ya kile walichokiona"

Numbers 13:27

kwa hakika ni nchi ya kutiririka maziwa na asali

"kwa hakika ni nchi nzuri kwa ufugaji na kilimo cha mazao" au " kwa hakika ni nchi yenye rutuba"

maziwa

"mazao ya yatokanayo na wanyama"

asali

"chakula kitokanacho na mazao"

Numbers 13:30

Kalebu

Kalebu alikuwa mmoja wa wapelelzi kumi na mbili ambao Musa aliwatumakuipelelza Kanaani.

tia moyo ... kutia moyo

Neno tia moyo au kutia moyo ni maneno ya kuwafariji na kuwahamasisha waendelee kufanya jambo fulani kwa ujasiri.

Numbers 13:32

wakasambaza taarifa ... waksema

Kiwakilishi cha "wa" kinamaanisha wale wanaume walioipelelza nchi isipokuwa Kalebu na Joshua.

Ile nchi waliyoipeleleza

Neno "wa" linamaanishawanaume wote walioipeleleza nchi akiwemo Joshua na Kalebu

nchi inayowala watu wake

"ni nchi ya hatari sana" au ni nchi ambayo hao watu watatuua"

Anaki

Hili ni jina la mwanaume

tulionekana ... machoni pao

"katika maoni yetu"

tulionekana kama mapanzi machoni mwao

"tulikuwa wadogo kama mapanzi ukitulinganisha nao"

Numbers 14

Numbers 14:1

Kwa nini BWANA alituleta katika nchi hii ili tufe kwa upanga?

"BWANA asingetuleta kwenye nchi hii ili tufe kwa upanga"

tufe kwa upanga

"tufe pale watu watakapotuvamia kwa upanga"

Je, si bora kwetu kurudi Misri?

Ingekuwa heri kwetu turudi Misri kuliko kujaribu kuwapiga Wakanaani"

Numbers 14:4

Wakasemezana wao kwa wao

Hii in amaanisha watu wa Israeli

kifudifudi

"wakalal kifudifudi ili kuonyesha unyenyekevu kwa Mungu" au "walilala kifudifudi ili kumwomba Mungu"

Numbers 14:6

Nuni .. Yefune

Haya ni majina ya wanaume

amabo walikuwa miongoni mwa wale waliokuwa wametumwa

Ambaowalikuwa miongonimwa wale ambao Musa alikuwa amewatuma

wakachana mavazi yao

kuchana mavazi ilikuwa ishara ya kuonyesha kuwa mtu huyo ametabika sana na anaomboleza

Ni nchi inayotiririka maziwa na asali

Tazama 13:27

Numbers 14:9

Sentensi unganishi

Joshua na Kalebu wanaendelea kuongea na watu

Tutawateketeza kwa urahisi kama kula chakula

"Tutawatekeza kwa urahisi kama tuwezavyo kula chakula

Ulinzi wao utakuwa umeondolewa

"BWANA atawaondolea ulinzi wao"

Ulinzi wao

"Yeyote ambaye atajaribu kuwalinda"

Numbers 14:11

Watu hawa watanidharau hadi lini? Wataendelea kutoniamini mpaka lini? nijapokuwa nimefanya ishara kwa nguvu zangu kati yao?

"Watu hawa wamenidhrau kwa muda mrefu. Wameshindwa kuniamiini kwa muda mrefukati, japokuwa nimefanya ishara ... kati yao

kuwaondolea urithi

"kuwakataa akuwa siwatu wangu" Hii inawez akumaanisha kuwa atawaangamiza.

kutoka kwenye ukoo wako

Kiwakilishi "wako" kinamaanisha Musa.

Numbers 14:13

uso wako umeonekana

Yaweza kumaanisha 1)Musa anaoakijionyesha kwa watu wake kama vile Mungunggea habari za Mungu amewaruhusu kuuona uso wake. "wamekuona" 2) Musa anaongelea ukaribu wa uhusiano wake na Mungu kama vile Musa humwona Mungu pale Mungu anapoongea naye. "wewe huongea moja kwa moja na mimi."

Numbers 14:15

kama mtu mmoja

kuwaua wote kwa wakati mmoja inaonekana kama kumwua mtu mmoja. "wote kwa wakati mmoja"

Numbers 14:17

kwa vyovyote vile atafutilia hatia

"yeye ataadhibu kwa sababu ya hatia"

atakapoleta hukumu ya dhambi za mababu juu ya wazao wao

"atakapoadhibu uzao wa watu wenye hatia kwa sababu ya hatia ya dhambi ya watu"

Numbers 14:20

dunia yoe itakapojazwa na utukufu wangu

"utukufu wangu utaijaza duia yote"

bado wamenijaribu

"wameendelea kunijaribu"

mara kumi

namba kumi inaonyesha mara nyingi. "mara nyingi sana"

hawakuisikiliza sauti yangu

"hawakutii kile nilichosema"

Numbers 14:23

Sentensi unganishi

BWSANA anaendelea kuongea na Musa

kwa sababu alikuwa na roho nyingine

neno "roho" linawakilisha mtazamo. "kwasababu alikuwa tayari kumtii Mungu" au "kwa sababu alikuwa na mtazamo tofauti."

Numbers 14:26

Nitaivumilia jamii ya watu hawa waovu wanaoninung'unikia mpaka lini

"Nimeivumilia jamii ya watu hawa waovu wanaoninung'unikia kwa muda mrefu."

Nimeyasikia malalamiko ya wana wa Israeli dhidi yangu

"Nimewasikia wana awa Israeli wakilalamika

Numbers 14:28

kama vile mlivyosema katika masikio yangu

"kama nilivyowasikia mkisema"

Maiti zenu zitaanguka

"mtakufa"

ninyi mliohesabiwa kwenye ile sensa

"Ninyi ambao Musa aliwahesabu kwenye ile sensa"

kuanzia umri wa mika ishirini na kuendelea

"umri wa miaka ishirini na zaidi"

Numbers 14:31

maiti zenu zitaanguka

"mtakufa"

Watoto wenu watakuwa wachungaji kwenye jangwa hili

"watoto wenu watazungukazunguka kwenye jangwa hili" kwa sababu wachungaji huzungukazunguka wakitafuta malisho.

Lazima watabeba madhara ya matendo yenu

"Lazima wapate mateso kwa sababu ya matendo yenu"

mpaka mwisho wa maiti ya mwisho

"mpaka wote mtakapokufa"

Numbers 14:34

mtabeba madhara ya dhambi zenu

"mtapokea madhara ya dhambi zenu"

Wao watakatwa kabisa

"wote wataangamizwa"

Numbers 14:36

Kwa hiyo wale wanume ... waliomlalamikia Musa

Matukio y a yaliyo kwenye 14:36 yamepangwa ili kwamba maana ieleweke kwa urahisi zaidi.

walikufa kwa tauni mbele ya BWANA

"walikufa mbele ya BWANA kwa tauni ambayo aliileta"

Numbers 14:39

Tazama

"Tazama" neno hili linaongeza msisitizo

Numbers 14:41

Kwa nini sasa mnapinga amri ya BWANA?

"Hampaswi kuwa mnapinga amri ya BWANA tena"

BWANA hayuko pamoja nayi

"BWANA hatawasaidia"

kuwalinda dhidi ya maadui zenu

"kuwalinda ili maadui zenu wasiwaangamize"

mtakufa kwa upnga.

"watawaua mtakapopigana nao"

mlimtega mgongo BWANA

"mliacha kumtii BWANA"

Hatakuwa pmoja nanyi

"hatawasaidia"

Numbers 14:44

walithubutu kukwea mlimani

"walithubutu kwenda mlimani hata kam ungu hakuwaruhusu"

mlimani

Sehemu kubwa ya nchi ya Israeli ni ya milima.Waisraeli walipovuka bonde Mto Yorodani ili kuivamia nchi ya Wakanaani, kulikuwa na milima ambayo walilazimika kuikwea ili waweze kwenda mbali zaidi ndani ya nchi ya Kanaani.

Numbers 15

Numbers 15:1

Taarifa kwa ujumla

Hesabu 15:1 -32 inaelezea kile ambacho Mungu alimwambia Musa awaambie wana wa Israeli

ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA ya ng'ombe au ya kondoo

"kumfurahisha BWANA kwa kuteketeza sadaka ya ng'ombe au ya kondoo"

Numbers 15:4

sadaka ya kuteketezwa

Tazama 15:4

Sehemu ya kumi ya efa

"lita 2"

robo ya hini

"takribani lita moja" au "lita 1"

Numbers 15:6

sehemu za kumi mbili za efa

efa moja ni kipimo kilicho sawa na lita 22. "lita 4" au "lita nne na nusu"

sehemu ya kumi ya efa

"karibu lita 2" au "lita mbili"

itatoa harufu nzuri kwa BWANA

"Mtampendezesha BWANA kwa kutoa sadaka hiyo"

Numbers 15:8

sehemu za kumi tatu

"lita tatu na nusu"

nusu ya hini

"lita mbili"

ilyotengenezwa kwa moto.

"ambayo mliiwekwa kwenye moto"

Ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA

Kumpendezsha BWANA kwa kutoa sadaka hiyo

Numbers 15:11

itafanyika hivi

"Lazima uifanye"

itafanyika kama ilivyoaanishwa

Lazma uifanye kama nilivyoainisha

iliyotengenezwa kwa moto

"ilitoteketezwa madhabhuni"

ili kufanya harufu nzuri kwa BWANA

"kumpendezesha BWANA kwa kutoa sadaka hiyo"

Numbers 15:14

lazima atoe sadaka iliyotengenezwa kwa moto

"Lazima ateketeza sadka madhabahuni"

ili kufanya harufu nzuri kwa BWANA

"Kumpendezesha BWANA kwa kutoa sadaka hiyo.

Ninyi mlivyo, ndivyo atakvyokuwa mgeni

maana yake yaweza kuwa 1) "Wewe na mgeni anayeishi na wewe mtakuwa sawa mbele ya BWANA" 2)"Sheria moja itakayotumika kw mgeni na kwako pia."

Atafanya kama mnavyofanya kwa BWANA

"atafanya kama mnavyofanya na kutii maagizo yote ya BWANA "

Numbers 15:17

chakula kitakachozalishwa katika nchi

"chakula kile ambcho nchi itazalishwa"

Numbers 15:20

mikate yenu ya kwanza

yaweza kumaanisha 1) mazao ya kwanza watakayokusanya wakati wa mavuno 2) Mikate ambayo itatengenezwa kutoka kwenye mavuno yao ya kwanza.

mkate

inapoitwa mkate mmoja ina maana kuwa walioka mkate kwanza

mtaiinua kwanza kama sadaka ya kuinuliwa

"kuiinua kama sadaka"

sadaka iloiyoinuliwa kutoka mahali pa kupuria nafaka.

Sadaka hii inafanywa kuwa sadaka kutoka mahali pa kupuria nafaka kwa sababu hapo ndipo mahali ambapo nafaka hutenganishwa na sehemu zingine za mmea.

Numbers 15:22

Sentensi unganishi

Mungu anendelea kumwmbia Musa kitu cha kuwaambia watu.

Taarifa kwa ujumla

Neno "m" linawakilisha waisraeli

ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA

Kumpendezsha BWANA kwa kutoa sadaka hiyo.

lazima itengenezwe sadaka ya unga nasadaka ya vinywaji

"lazima mtengeneze sadakaya unga na sadaka ya vinywaji"

kama ilivyoagizwa katika amri

"kama amri inavyoagiza"

Numbers 15:25

Watasamehewa

"Nitawasamehe"

iliyotengenezwa kwa moto

"ambayo waliitengeneza kwa moto"

Ndipo watu wte wa Israeli watasamehewa"

"Nitawasamehe jamii yote ya watu wa Israeli"

Numbers 15:27

mbuzi jike wa umri wa mwka mmoja

"mbuzi jike wa umri wa mwka 1"

Yule mtu atasamehewa baada ya upatanisho kufanyika

"Nitamsamehe mtu yule baada ya kuhani kufanya upatanisho"

Numbers 15:30

Huyo mtu ataondolewa kati ya watu wake

Yaweza kumaanisha 1)" watu wake watamfukuza 2) "sitamtambua tena kuwa sehemu ya watu wa Israeli 3) "watu wake lazima watamwua."

amevunja amri yangu

"ameshindwa kutii amri yangu"

Dhambi yake itakuwa juu yake

Hapa "dhambi" inamaanisha 1) adhabu kwa ajili ya dhambi 2) hatia ya dhambi hiyo. dhambi kuwa juu yake ni sitisri inayomaanisha 1) kuadhibiwa 2) kuwa na hatia. kwa hiyo, Nitamwadhibu kwa sababu ya 1)dhambi zake au 2) Nitamwonw kuwa ni mwenye hatia.

Numbers 15:32

kwa sababu ilikuwa haijamriwa atakchotendewa

"BWANAalikua hajatamka cha kumfanya huyo mtu"

Numbers 15:35

Yule mwanamume lazima auawe

"kwa hakika lama mwue mtu huyo"

Numbers 15:37

wana wa Israeli

Israeli lilikuwa jina jingine la Yakobo. "watu wa Israeli"

na kuzishika

"kuzitii"

ili kwamba msije mkatangatanga katika mioyo yenu na macho yenu

"ili kwamba msije mkafikiria chochote manchokitaka"

na kuwa waasherati kwa hayo

"na kwa aibu mkashindwa kuw waaminifu kwangu"

Numbers 15:40

Sentensi unganishi

Mungu anaendeles kumwambia Musa vitu vya kuwawambia Waisraeli. Neno "fa" linawahusu Waisraeli.

kukumbuka

"kukumbuka

Mimi ndimi BWANA Mungu wenu

Kirai hiki kinajirudiaili kutoa msisitizo

Numbers 16

Numbers 16:1

Kohathi

Tazama 3:17

Wakamwinukia Musa

"walimpinga Musa"

mia mbili na hamsini

"250"

waliokuwa wakifahamika katika ile jamii

"watu wa muhimu katika ile jamii"

mnatumia mamlaka zaidi ya uwezo wenu

"Mmefanya zaidi ya kile manchotakiwa kufanya"

Kwa ini mnajiinua sana juu ya watu wengine wa BWANA?

"Mmekoswa kujiinua wenyewe juu ya watu wengine wa BWANA"

mnajiinua sana juu ya watu wengine

"mnajiona wenyewe kuwa wa mhimu kulikowengine"

Numbers 16:4

akalala kifudifudi

Hii inamanisha kuw Musa alikuwa akinyenyekeza kwa Mungu. Musa aliogopa kuwa Mungu angewaadhibu watu waliokuwa wanampingaMungu na viongozi wake aliokuwa amewachagua

aliyetengwa kwa ajili yake

"ambaye BWANA amemtenga kwa ajili yake"

Numbers 16:6

Sentensi unganishi

Musa anaendelea kuongea na Kora na wale wanaume waliokuwa na kora

vyetezo

vyombo vya kufukizia uvumba

mbele za BWANA

"katika uwepo wa BWANA"

yule ambye BWANA atamchagua atamtenga kwa BWANA

"BWANA atamenga mtu huyo kwa ajili yake"

Mmeenda mbele zaidi

"Mmefanya za"idi ya kile mnachotakiwa kufanya" au "Mmechukua mamlaka zaidi ya kiasi mnachotakiwa

Numbers 16:8

Je, ni jambo dogo kwenu... ili muwatumikie

"mnaishi kana kwamba ni jambo dogo kwenu ... kuwatumikia"

ni jambo dogo kwenu

"haitoshi kwenu" au "siyo mhimu kwenu"

mnataka na ukuhani pia

"mnataka na huduma ya ukuhani pia" au "mnataka kuwa makuhani pia"

kwa nini mnalalamika juu ya Haruni, ambaye anamtii BWANA?

"Kiuhalisia hamumlalamikii Haruuni, bali BWANA, ambaye Haruni anamtii"

Numbers 16:12

Kwani ni jambodogo kwamba umetuleta mpaka ... ili kutuua kwenye jangwa

"mnadhani ni jambo dogo kwamba umetuleta ... ili kutuua katika jangwa hili."

ni jambo dogo

"haitoshi" au "isiyo na umhimu"

nchi ya kutiririka maziwa na asali

tazama 14:6

kutupa urithi

Inahusisha kile ambacho Mungu atawapa kuwa mali yao milele kama urithi wao

Sasa unataka kutuposha na ahadi hewa?

"Sasa unataka kutuposha na ahadi hewa."

kutupofusha

"kutudanganya"

kwa ahadi hewa

"kwa ahadi ambazo huwezi kuzitimiza"

Numbers 16:15

Sijachukua punda mmoja kutoka kwao

"Sijachukua chochote kutoka kwao, wala hata punda mmoja"

vyetezo

vyombo vya kufukizi uvumba

Numbers 16:18

moto

moto ni joto, mwanga, miali ambayo hutokea wakati kitu fulani kinapochomwa. Moto pia hutumika kwa maana ya utakaso au hukumu.

hema ya kukutania

Hii ni hema ambayo ya mud ambayo Mungu aliitumia kukutana na Musa kabla ya kujengwa ile masikani. Hema ya kukutania iliwekwa nje ya kambi. Wakati mwiingine neno "hema ya kukutania" ilitumika kumaanisha masikani. Baada ya Waisraeli kujenga masikani; ile hema ya kukutania haikuwepo tena.

Musa

Huyu alikuwa nabii na kiongozi wa Waisraeli kwa muda wa miaka 40

Haruni

Huyu alikuwa kaka mkubwa wa Musa. Mungu alimchagua Haruni kuwa kuhani mkuu wa kwanza wa watu wa Israeli

Kora

Kora ni jina la wanaume watatu katika Agano la kale. Wa kwanza ni yule mwana wa Esau ambaye baadaye alikuja kuwa kiongoziwa watu wake. Wa pili ni yule aliyekuwa wa uzao wa Lawi ambaye pia alitumika kwenye masikani kuhani na baadaye kumwonea wivu Musa naHaruni na alikuwa nakundi la wanaume waliowapinga. Wa tatu ni yule alyeorodheshwa kama kwenye ukoo wa Yuda.

BWANA (YAHWEH)

BWANA ni jina binafsi la Mungu ambalo alilifunua wakati aliapoongea na Musa kwenye kile kichaka kilichokuwa kinawaka moto. Neno hili YAHWEH linatokana na neno linalomaanisha "kuwepo" au "kuishi." Maana halisiy aweza kuwa "Yeye ndiye" au "Mimi ndiye" au "Yeye anyewezesha kuwepo."

utukufu

Neno "utukufu" linamanisha heshima, fahari, na ukuu uliotukuka. Wakati mwingine utukufu humaanisha kitu chenye thamani kubwa na cha muhimu. na Kwa mukhutadha mwingine inaweza kumaanisha mng'ao au hukumu.

Numbers 16:20

ili nipate kuwaangamiza

"ili niweze kuwatekeketeza"

wakalala kifudifudi

Hii inaonyesha kuwa Musa na Harunu walikuwa wnajinyenyekeza

Mungu wa wote wenye mwili

"Mungu anayewpa watu uhai"

kama mtu akitenda dhambi, ni lazima uwe na hasira na watu wote?

"tafadhali usiwe na hasira na watu wote kwa sababu ya dhambi ya mtu mmoja."

Numbers 16:23

hema

Hema ni kibanda kinachobebeka amacho kimetengenezwa kwa nyuzi zilizosukwa na zinazowezwa kuunganishwa na nguzo ndogo ndogo pamoja. hema zinaweza kuwa ndogo ndogo au kubwa kubwa.

Numbers 16:25

mtaangamizwa

"mtateketezwa"

mtataanganizwa na dhambi zao

"mtateketezwa kwa sababu ya dhamabi zao zote"

mtataanganizwa na dhambi zao

"mtateketezwa kwa sababu ya dhamabi zao zote"

Numbers 16:28

ndipo mtakapojua

"ndipo" inamaanisha kile ambcho Musa atakisema baadaye

ambye huwameza kama mdomo mkubwa

"na wataangui ndani yake na kufunikwa ndani yake"

Numbers 16:31

Dunia ikafungua makanwa yake na kuwameza

"Dunia ikafungua makanwa yake naowkaangukia ndani yake na kuwafunika"

Numbers 16:33

wakaingia ndani shimoni wakiwa hai

tazama 16:28

wakashangaa

kiwakilishi "wa" kinawakilishsa Waisraeli"

Nchi isije kutumeza na sisi pia

"Nchi inaweza kufunguka na sisi pia tukaangukia ndani yake na kufunikwa" au "Nchi ikifunguka tena na sisi tutangukia ndani yake tukaangukia ndani yake"

Kisha moto ukashuka toka kwa BWANA ukawaangamiza wale wanaume 250

"Moto ukawaka kutoka kwa BWANA ukawaangamiza wale wanaume 250"

Numbers 16:36

kutoka ule moto

Hii inamaanisha ule moto uliowaangamiza wale wanaume 250

wale waliopoteza maisha

"wale waliokufa"

Na vifanyike

"Na Eliezeri atavifanya"

ni vitakatifu. Vitakuwa ishara

"vi" na "vi" inamaanishsa vile vyetezo

Numbers 16:39

vilikuwa vimetumiwa na wale watu walioungua

"vile ambavyo wale wanaume walioungua kwa moto walikuwa wamevitumia."

ili wasje kuwa kama Kora na kundi lake

"wakafa kama Kora na kundi lake walivyokufa"

Numbers 16:41

Kisha ikatokea

Kirai hiki kimetumika hapa kuonyesha tukiola muhimu sana katika simulizi hili.

walipokuwa wamekusanyika kinyume na Musa.

"walikuwa wamekusanyika ili kumnung'unikia Musa na Haruni"

tazama

"ghafla." Neno hili limetumika ili kuonyesha kuwa watu walishangazwa na kile walichokiona.

Numbers 16:44

ili niwaangamize

"ili kwamba niweze kuwaangamkiza"

wakalala chini kifudifudi

Hii inaonyesha kuwa Musa na haruni walijinyenyekeza mbela za Mungu.

hasira hii inatoka kwa BWANA

"BWANA antuonyesha hasira zake"

Numbers 16:47

akaweka ndani yake uvumba

"akachoma uvumba"

ile tauni ikazuiwa

"ile tauni ikazuiawa kuenea"

Numbers 16:49

Kora

Tazama 16:19

Hema ya kukutania

Tazama 16:18

Numbers 17

Numbers 17:1

kumbi na mbili

"12"

Numbers 17:3

Sentensi unganishi

BWANA anaendelea kuongea na Musa

Fimbo ya Lawi

"Jina la Lawi hapa linamanisha kabila ya Lawi

kwa kila kiongozi kutoka kwenye kabila la mababu zao

kiwakilishi "zao" kinamaanisha "kwa kila kiongozi"

amri za agano

Kirai cha "amri za agano" inamaanisha "sanduku la amri za agano" au "sanduku la amri za agano"

fimbo ya mtu yule ninayemchagua itachipua

"machipukizi yataanza kukua katika fimbo ya mtu yule nitakayemchagua"

Nitazuia watu wa Israeli walalamikao, ambao ambao wanaongea kinyume na wewe

"nitawafanya watu wa Israeli waache kulalamika dhidi na yako"

Numbers 17:6

aliyechaguliwa kutoka kwenye kila kabila

"ambaye Musa alimchagua kutoka kwenye kabila la mababu"

katika hema ya amri ya agano

"hama ya sanduku la agano"

Numbers 17:8

na tazama

Neno "tazama" linaonyesha kuwa kuna kitu cha muhimu kimetokea.

Numbers 17:10

amri za agano

"sanduku la agano"

ili ukomeshe malalamiko

"ili kwamba uwazuie kukulalamikia"

vinginevyo watakufa

"ili wasijekufa"

Numbers 17:12

tutakufa hapa. Wote tutaangamia

Virai vyote viwili vinvamaanisha kitu kile kile na vimetumika ili kuonyesha msisitizo.

Numbers 18

Numbers 18:1

dhambi zote zilizotendwa mahali patakatifu

"dhambi zote ambazo mtu amezifanya dhidi ya mahali patakatifu"

kwa uovu wowote uliofanywa na yeyote mahali patakatifu

"dhambi zote ambazo mtu huzifanya akiwa mahali patakatifu"

yeyote mahali patakatifu

"kuhani yeyote"

Numbers 18:3

Sentensi unganishi

BWANA anaendelea kuongea na Haruni.

Watakutumikia ... Wataungana na wewe

kiwakailiashi "wa" kinamaanisha Walawi. Na kiwakilishi "wewe" kinamwakilisha Haruni.

vinginevyo wewe na wao mtakufa

kiwakilish "wao kinamaanisha mtu yeyote katika kabilla Walawi anayesogelea kitu chochote mahali patakatifu. Kiwakailishi "wewe" kinamaanisha"Haruni" na Walawia wengine wanaotumika katika maeneo yaliyoidhinishwa.

asikusogelee. Wewe utaajibika.

kiwakilishi cha "wewe" ni cha wingi kinachomwakilisha Haruni na walawi wengine.

ili kwamba hasira yangu isiwajilie watuwa Israeli tena.

"ili kwamba nisije nikwaadhibu Waisraeli tena."

Numbers 18:6

Sentensi unganishi

BWANA anaendelea kuongea na Musa tena

Wao ni zawadi kwako

"Wao ni kama zawadi kwako.

waliotolewa kwangu

Neno "waliotolewa" kwa Mungu inamaanisha waliotengwa ili wamtumikie Mungu. "Ambao nimewatenga kwa ajili yangu"

wewe pekee yako na wanao

Kiwakilishi "wewe" na "yako" vinamaanisha Haruni na wanawe

kufanya kazi ya ukuhani

"kufanya kazi ya ukuhani"

kitu chchote ndani ya ukuhani

"kitu chochote chumbani nyuma ya lile pazia"

Mgeni yeyote anayekaribia atauawa

"Mgeni yeyote anayekaribia atakufa" au "mtamwua kila mgani anayekaribia"

anayekaribia

"anayekaribia maeneo matakatifu"

Numbers 18:8

Sadaka za kuinuliwa kwangu

Kirai cha "Kuinuliwa kawngu" knamaaisha kutoa kitu kwa Mungu. "Sadaka ambazo watu hutoa kwangu"

Nimekupa sadaka hizi wewe

"Nimeshazitoa sadaka hizi kwako"

kuwa haki yako milele

"kuwa sehsmu ya urithi ambayo utaendelea kupata"

visiteketezwe kwa moto

"amabvyo havitateketezwa kabisa kwa moto madhabahuni"

ni vitu vitakatifu sana

"vitu hivi ni vitskstifu sana"

Numbers 18:10

Sentensi unganishi

Mungu anaendelea kuongea na Haruni.

ambaye ni msafi

"anayekubalika kwangu"

Numbers 18:12

Sentensi unganishi

Mungu anaendelea kuongea na Haruni

Mavuno ya kwanza

Hii inamaanisha mafuta yale mazuri ya kwanza

Kila mtu aliyemzuri kwenye familia yako

"Kila mtu kwenye familia yako anayekubalika kwangu"

Numbers 18:14

Sentensi unganishi

Mungu anaendelea kuongea na Haruni

Kila kitu kinachofungua tumbo, kila limbuko

"kila mzaliwa wa kwanza wa kiume"

Kila kitu kinachofungua tumbo

Nahau hii ya "kufungua tumbo" mzaliwa wa kwanza wa kiume ambaye mama huzaa"

watu lazima wawakomboe wazaliwa wa kwanza wa kiume

Badala ya kutoa sadaka wazaliwa wao wa kwanza, watu walitakiwa kuwalipa makuhani kwa ajili ya wana wao.

Wale ambao wanahitaji kukombolewa na watu watakombolewa wakiwa na umri wa mwezi mmoja

"watu watawakomboa wakiwa na umri wa mwezi mmoja."

Wale wanaohitaji kukombolewa

Hii inamaanisha watu ambao wanatakiwa kukombolewa na wala si wale wanyama ambao ni wazaliwa wa kwanza wasiosafi

shekeli tano .... ambazo ni sawa na gera ishirini

""vipande vitano vya fedha ... ambvyo kila kimoja ni sawa na gramu ishirini za fedha" au "gramu hamsini za fedha kwa kipimo cha mahali patakatifu"

shekeli tano

Shekeli moja ni kipimo cha uzani. "shekeli tano za fedha"

shekeli za mahali patakatifu

Hizi ni shekeli zenye uzani tofauti. Ni kipimo ambacho kilitumikaa kwa mahali patakatifu hemani. Uzani wake ulikuwa gera ishirini sawa na gramu 11.

Numbers 18:17

Sentensi unganishi

Mungu an endelea kuongea na Haruni

Utanyunyizia damu yake

"mtawachinja na kunyunyizia damu yake"

sadaka ya moto

"ambayo imetengenezwa kwa moto"

harufu nzuri ya kumpendeza BWANA

"BWANA atapendezwa nanyi"

kidali cha kuinuliwa na paja la kulia

"kidali na paja la kulia ambalo utaliinua kama sadaka kwangu"

Numbers 18:19

Sentensi unganishi

Mungu anaendelea kuongea na Haruni

nimekupa wewe

"Ninakupatia wewe"

Kama gawio la kudumu

"Kama sehemu ambayo mtaendelea kupata"

Hili ni agano la milele la chumvi. Agano linalofunga milele

"mapatano aya milele"

agano la milele la chumvi

"agano lililotengenezwa kwa chumvi." Chumvi inawakilisha kitu cha kudumu na ilitumika kwa ajili ya sadaka kwenye chakula cha maagano. "agano la kudumu" au " agano la milele"

wala hautakuwa na gawio miongoni mwa watu

"Hautamilikishwa ardhi ya watu" au " au hauatapokea chochotekatika ardhi ambayo Waisraeli wataimiliki"

Mimi ndio gawio lenu na urithi wenu

"Badala yake Mimi ndio nitakuwa kile matakachohitaji" au " Badala yake, Mimi nitawaruhusu kunitumikia na nitatoa kwa ajili yenu kupitia huduma hiyo"

Numbers 18:21

Sentensi unganishi

Mungu anaendelea kuongea na Haruni

Tazama, Nimewapatia

"Neno "tazama" linaongeza msisitzo wa kile kinachofuata. "kwa hakika, Nimwewapeni"

kuwa urithi wao

"kama sehemu ay kile ninachowapatia Waisreali wote"

Numbers 18:23

Sentensi unganishi

Muungu anaendelea kuongea na Haruni

Na miongoni mwa watu wa Israeli hawa hawatakuwa na urithi.

"Hawatakuwa na ardhi yeyote ambayo watu wengine wa Israeli watapewa"

kuwa urithi wao

"kama sehemu ambayo ninawapa Waisraeli wote"

Numbers 18:25

Mnapopokea zaka tokakwa watu ambayo BWANA amewapa

Watu wa Israeli walikuwa wakimtolea BWANA ehehemu ya kumi ya mazao na ya wanyama, na BWANA aliwapatia hiyo Walawi

kuwa urithi

"kama seheelimu ya kile ninachowapita Waisraeli wote"

Zakayenu itahesabika kama moja ya mapato

"mkumbuke kutoa"

Numbers 18:28

Sentensi unganishi

Mungu anaendelea kumwambia Musa kile anachopaswa kuwaambia watu

mtatoa mchango wenu kwa Haruni yule kuhani

"mtampa Haruni yule kuhani mchango ambao BWANA anawadai"

ambavyo mmepewa

"vile ambvyo watu wa Israeli wamewapeni"

Numbers 18:30

Sentensi unganishi

Mungu anaendelea kuongea na Musa

hayo matoleo mazuri

"hayo matoleo m azuri ambayo mmepokea toka kwa watu wa Israeli"

nafaka zote zinazobaki

"nafaka" haya nimatoleo ambayo watu wa Israeli humpa Mungu na Walawi huzipokea.

Hamtakuwa na hatia yeyote kwa kuvila na kuvinywa

"hamtakuwa na hatia pale mtakapovila na kuvinywa"

Numbers 19

Numbers 19:1

ni amri, ni sheria

Maneno haya mawili yanamaanisha kitu kilekile. "Ni amri za kimahakama"

wakuletee

Neno "wa" inamlenga Musa

kipaku wala waa

maneno haya yana maana ileile, yametumikaa pamoja kuongeza msisitizo kuwa mnyama huyu anatakiwa kutokuwa na dosari yeyote"

Numbers 19:3

mbele ya macho yake

"akiwa anaona" au "mbele yake"

yule kuhani atachukua mtia wa mwerezi

kuhania anayesemwa hapa ni Eliezeri

sufu

"sufu nyekundu"

Numbers 19:7

atafua nguo zake

"neno "a" linamwakilisha Eliezeri yule kuhani

Naye atabaki najisi

Hatakubalika kwa Mungu asiyefaa kufanya kazi yeyote. Mtu wa jinsi hii ni najisi.

Numbers 19:9

mtu aliyesafi

Mtu aliyesafi na anayeweza kufanya takatifu alihesabiwa kuwa ni msafi.

Majivu haya yatatunzwa

"Mtatayatunza haya majivu"

kwenye eneo safi

Kukubalika kwa kunamaanisha kuwa msafi. "Eneo linalokubalika"

atabaki najisi

Kutokukubalika kwa Mungukulionyesha kutoruhusiwa kufanyakazi yeyote takatifu. Ni ile hali ya kutokuwa msafi.

Numbers 19:11

Taarifa kwa ujumla

wazo la "usafi" na "Utakatifu" linamaanisha kukubalika kwa Mungu

Taarifa kwa ujummla

wazo la "unajisi" na "uchafu," "kutokuwa msafi"linamaanisha kutokukubalika kwa Mungu.

maiti

"mwiliya mtu aliyekufa"

lakini kama hajajitakasa

"aomba mtu wa kumtakasa"

lakini kama hajajitasa mwenyewe katika siku ya tatu, basi hatakuwa safi katika siku ya saba

"atakuwa safi siku ya saba tu iwapo kama atajitakasa siku ya tatu"

mtu huyo ataondolewa

tazama 9:13

maji ya farakano yalikuwa hayajanyunyiziwa kwake

"hakuna alimnyunyizia maji ya farakano"

Atabaki najisi; na unajisi wake utabaki kwake

Virai hivi viwili vinamaanisha kitu kilekile. Vimetumika kwa pamoja kuonesha msisitizo

Numbers 19:14

Taarfa kwa ujumla

Lile wazo la "unajisi" linamaanisha kutokukubalika kwa Mungu au kutokuwa tayri kwa matumizi.

Kila chombo ambacho hakiina kifuniko kinanjisika

"vyombo amabvyo havina vifuniko vitabaki kuwa najisi kama havina vifuniko"

mtu aliyeuawa kwa upanga

"mtu ambaye aliuawa kwa upanga na mtu mwingine"

Numbers 19:17

Taarifa kwa ujumla

Lile wazo la "unajisi ni ile hali ya kutokukubalika kwa Mungu au kutokuwa tayari kwa matumizi

Taarifa kwa ujumla

Lile wazo la "usafi" na "utakatifu" linamaanisha kukubalika kwa Mungu

Numbers 19:20

Taarfa kwa ujumla

Lile wazo la "unajisi ni ile hali ya kutokukubalika kwa Mungu au kutokuwa tayari kwa matumizi

Taarifa kwa ujumla

Lile wazo la "usafi" na "utakatifu" linamaanisha kukubalika kwa Mungu

Huyi mtu ataondolewa

Tazama 9:13

Hajanyunyiziwa maji ya utakaso

"hakuna alimnyunyizia maji ya utakaso"

maji ya ufarakano

Tazama 19"11

Numbers 20

Numbers 20:1

Jangwa la Sini

Neno "Sini" ni neno la Kihebrania la jangwa.

mwezi wa kwanza

Huu ni mwezi wa kwanza wa Kalenda ya Kihebrania. unaoanza wakati Mungu aliwakomboa kutoka kwa Wamisri. Mwezi huu ulikuwa kati ya mwezi Machi na mweziwa Aprili katika Kalenda yetu ya Kimagharibi

alipozikwa

"na wakamzika"

Numbers 20:2

wakakusanyika

"kiwakilishi "wa"kinamaanisha watu wote

wakakusanyika pamoja

"walikuja pamoja kama kundi"

mbele ya BWANA

Hii inamaanisha kuwa mbele ya hema ya BWANA

Numbers 20:4

Sentensi unganishi

Watu wa Israeli wanaendelea kulalamika mbele ya Musa na Haruni

Kwaa nini umewaleta watuwa BWANA ... sisi na wanayama wetu?

"ni bora kama watu wa BWANA katika jangwahili ili kufa,hapa, sisi na wanyama wetu."

Kwa nini ulitutoa Misri ukatuleta katika eneo hili baya?

"Ni bora kama usingetutoa Misrina kutuleta katiaka eneo hili baya."

Numbers 20:6

wakalala kifufudifudi

Hii inaonesha kuwa Musa na Haruni walikuwa wakijinyenyekeza kwa BWANA.

Numbers 20:7

mbele ya macho yao

kiwakilishi cha "yao" kinaonesha watu waliona kile ambacho Musa alifanya. "wakati wakiona"

akachukua hiyo fimbo mbele ya BWANA

"mbele ya hema ya BWANA"

Numbers 20:10

Lazima tuwape amaji kutoka kwenye huu mwamba?

"Hamkufurahi ingawa tuliufanya mwamba huu kutoa maji, hata hivyo nitafanya"

Lazima tulete

"Kiwakilishi "tu" kinamwakilisha Musa na Haruni na kiaweza kumjumuisha BWANA, hakijumuishi wale watu wengine.

Numbers 20:12

Kwa kuwa hamkuniheshimu mimi na kuniamini mbele ya macho ya Israeli

"Kwa kuwa hamkuniheshimu mimi na kuniamini mbele ya macho ya Israeli kama mtakatifu, lakini niliumpiga ule mwamba badala ya kuuambia kama nilivyoawaambia"

mbele ya watu wa Israeli

"wakati watu wa Israeli wakikutazama wewe"

Mahali hapa paliitwa

"watu walipaita mahali hapa"

Numbers 20:14

Ndugu yako Israeli

Musa anatumia Kiraihiki ili kusisitiza kuwa Waisraeli na Waedomu walikuwa na uhusiano kwa sababu mababu zao Yakobo na Esau walikuwa ndugu.

Tulipomlilia BWANA

"Tulipomwomba BWANA atusaidie"

akatusikia sauti zetu

Neno "sauti" linawakilisha kilio au kile ambacho watu walimwambia. "alisikia kilio chetu" au "alitusikia kile tulichomwomba"

Tazam

Neno "Tazama" hapa linamaanisha kubadilisha mada. Walikuwa wanaongelea mambo yao ya nyuma na sasa wanaongelea mambo yao ya sasa ili wakati wanajiandaa kumwomba mfalme ili afanye kitu.

Numbers 20:17

Sentensi unganishi

Wale watumishi wanaendelea kuongea na mfalme wa Edomu

Hatutageuka upande wa kulia wala wa kushoto

Neno "kugeuka" linamaanisha kuiacha barabara, "Hatutaiacha barabara kwa uelekeo wowote"

nia kuu ya mfalme

Hii ni barabara kuu inayounganisha mpaka Dameski hadi Kaskazini kwenye ghuba ya Akabahi.

Numbers 20:18

Msipite hapa ... nitakuja na upanga na kukuvamia

"watu wako wasipite hapa ... kuwavamia"

Nitakuja na upanga

"Nitatuma jeshi langu"

Watu wa Israeli

Hii inamaanishsa wale watu wa Israeli waliokuwa wametumwa

tukitembea kwa miguu

Inamaanisha kuwa watapita kwenye hilo eneo wakitembea.

Numbers 20:20

kwa hiyo mfalme wa Edomu akawa kinyume cha Israeli kwa mkono wenye nguvu pamoja na jeshi kubwa sana.

"mfalme wa Edomu akatuma jeshi kubwalenye askari wengi ili kuwavamia Waisraeli"

kupita kwenye mipaka yake

Neno "yake" linamaanisha Waedomu

Numbers 20:22

Wana wa Israeli, watu wote

Kirai cha "watu wote" kinasisitiza kuwa kia mtu aliyekuwa sehemu ya Waisraeli alikuwepo bila kuwa na udhuru

Haruni kukusanyika na watu wake

Hii ni tafsida ya kusema kuwa Haruni atakufa. Ni wakati wa Haruni kufa na roho yakae kwenda mahali walipo mababu zake. "Haruni atakufa"

hamkutii sauti yangu

"sauti yangu" inamaanisha kile ambacho Mungu alikuwa amesema," Mlikataa kufanya nilichokuwa nimeema"

Numbers 20:25

Sentensi unganishi

Muungu anaendelea kuongea na Musa

atakufa na kulazwa pamoja na watu wake

Ni wakati wa Haruni kufa na roho yake kwenda walipo mababu zake

Numbers 20:27

siku thelathini

"siku 30"

Numbers 21

Numbers 21:1

akapigana dhidi ya Israeli

"Majeshi yake yakapigana dhidi ya Waisraeli"

Israeli akaapa

"watu wa Israeli wakaapa" au "Waisraeli wakafanya kiapo"

BWANA akaisikia sauti ya Israeli

"alifanya kile Israeli alichoomba"

sauti ya Israeli

ambacho Israeli aliomba

Wakawaangamiza kabisa pamoja na miji yao

"Watuwa Israeli wakaliangamiza kabisa jeshi la Wakanaani na miji yao"

Mahali pale paliitwa Horima

"Wakapaita mahali pale Horima"

Numbers 21:4

Kwa nini umetutoa Misri ili tufe katika jangwa hili?

"Usitutoe Misri ili tuje kufa katika jangwa hili"

Numbers 21:6

Tumemnung'unikia Musa na wewe

"Tumesema mabo mabya juu ya BWANA na wewe"

Tu

Kiwakilishi "tu" kinawakilisha watu wa Israeli bila kumjumuisha BWANA na Musa.

Numbers 21:8

Tengeneza nyoka

"Tengeneza mfano wa nyoka"

kila anayeumwa

"kila amabaye ataumwa na nyoka

nyoka wa shaba

"nyoka anayetokana na shaba"

na kumwanagalia huyo nyoka atapona

kiwakilishi "a" kinmwakilisha mtu yeyote aliyeumwa na nyoka.

Numbers 21:10

linalokabili Moabu

"ambalo linafuatia Moabu"

Numbers 21:12

ndio unaotengeneza mpaka wa Moabu na Amoni

Hii inamaanisha kuwa hawa watuwaliishi katika maeneo mwaili tofauti katika ule mto, amabayo mto ulikuwa mpaka wao.Wamoabu walishi kusini mwa mto na Waamori walishi upande ule wa Kusini.

Numbers 21:14

Wahebu katika Sufa

haya ni majina mawili ya mahali pale

mtelemko wa bonde linaloelekea katika mji wa Ari na kuelekea kwenye mpaka wa Moabu

"mtelemko unaoelekea kwenye mji wa Ari na mpaka wa nchi ya Moabu

Numbers 21:16

mpaka Beeri, hapo ndipo palipo na kisima ambacho

"mpaka Beeri. Hapo palikuwa na kisima"

ambacho BWANA almwambia Musa, "Wakusanye watu kwa ajili yangu ili uwape maji,"

"mahali ambapo BWANA alimwambia Musa kuwakusanya watu pamoja ili awape maji"

Numbers 21:17

enyi visima, yajazeni maji

"enyi maji, vijazeni visima"

Kisima ambacho viongozi wetu walichimba, kisima ambacho wenye hekima walichimba

Virai hivi viwili vivnamaanisha kitu kile kile, vimetumika kusisitiza wajibu wa viongozi kwa jukumu la kuchimba visima.

kwa fimbo ya kifalme na kwa fimbo ya kutembelea

"wakitumia hata fimbo zao za kifalme na za kutembelea"

Numbers 21:19

Nathalieli ... Bamothi

Haya ni majina ya maeneo

Mlima Piska

Hili ni jina la Mlima

kinapoonekana jangwani

"kinatokezea kutoka jangwani"

Numbers 21:21

Kisha Israeli

"Israeli" inamaanisha watu wa Israeli, hasa viongozi wao. "kisha Waisraeli"

Hatutapita kwenye shamba lolote au shamba la mizabibu

"Hatutaingia kwenye shamba lenu lolote au shamba la mizabibu"

njia kuu ya mfalme

Tazama 20:17

kupita kwenye mpaka wao

"kuvuka mpaka wao." Neno "wao" linamaanisha Waamori

Jahazi

Hili ni jina la mahali

alipigana dhidi ya Israeli

kiwakilishi "a" kina mwakilisha jeshi la Mfalme Sihoni, "jeshi lake lilipigana dhidi ya Israeli"

Numbers 21:24

Israeli akalivamia

Neno "Israeli" linamaanisha Waisraeli. "Waisraeli wakawavamia"

kwa nchaya uoanga

"na wakawaangamiza kabisa"

na kuchukua nci yao

"wakaitwaa nchi ya Waamori"

Watu wa Amoni ... Waamori

"Waamoni ... Waamori" au "watu wa Amoni ... watu wa Amori" majiina haya yanafanana lakinai yanamaanisha watu wa makundi mawili tofauti.

ulikuwa umefungwa

"ulikuwa na ulinzi imara"

Heshiboni na vijiji vyake vyote

"Hshiboni na vijiji jirani alivyovitawala"

Sihoni alikuwa ameteka ardhi yake yote

Neno "yake" linawakilisha mfalme wa Moabu.

Numbers 21:27

Heshiboni ... mji wa Sihoni

Haya ni majiina mawili yanayomaanisha mji uleule

Mji wa Sihoni ujengwe na kuimarishwa tena

"Mtu aujenge mji wa Sihoni na kuimarisha tena mji wa Sihoni"

Moto uliwaka toka mji wa Heshiboni, moto kutoka mji wa Sihoni

"Mfalme Sihoni alikuwa na jeshi imara kutoka mji wa Heshiboni"

Uliteketeza Ari ya Moabu

"uliharibu mji wa Ari katika nchi ya Moabu"

Numbers 21:29

Moabu ... watu wa Chemoshi

Virai hivi vinamaanisha watu walewale

Watu wa Chemoshi

"Chemoshi" lilikuwa jina la mungu wa Uogo amabye aliabudiwa na Wamoabu. "watu waliomwabudu Chemoshi"

Amewafanya watu wake

kiwakilishi "a" na "wake" kinamaanisha Chemoshi

tumewapiga

kiwakilishi "tu" kinawawakilisha Waisraeli waliompiga Sihoni

Tumeiangamiza Heshiboni

"Tumeiangamiza Heshiboni"

Heshiboni ...mpaka Diboni. Mpaka Nofa ... Madeba

Maeneo yote haya yako kwenye ufalme wa Sihoni. Hii inamaanisha kuwa Waisraeli waliuangamiza utawala wote wa Sihoni.

Numbers 21:31

kuwafukuza

"waliwaondosha"

Numbers 21:33

akatofautiana nao

"aliwavamia"

Mfanyeni kama mlivyomfanya Sihoni

"Mwangamizeni kama mlivyomwagamiza Sihoni mfalme wa Waamori"

Kwa wakamwua

"Kwa hyo jeshi la Israeli likamwua Ogu"

wote wakaisha na hakubaki hata mmoja aliyebaki hai

"watu wake wote waliuawa"

wakaichukua nchi yake

"wakaitawala nchi yake"

Numbers 22

Numbers 22:1

kwenye upande mwingine wa mto Yorodani kutoka mji ule

Waisraeli walikuwa wameweka kambi uoande wa Mashariki wa mtoYorodani. Yeriko ilikuwa magaharibi mwa mto

Numbers 22:2

Baalaki mwana wa Zippori

Balaki alikuwa mfalme wa Moabu

Moabu aliwaogopa sana hao watu ... Moabu aliwahofia wana wa Israeli

Virai vyote viwili vinamaanisha kitu kilekile na vimetumika kuonesha jinsi Moabu alivyokuwa amaeogopa

Moabu aliogopa sana

"Wamoabu wote walikuwa wameogopa sana"

Kwa sababu walikuwa wengi sana

"Kwa sabau ya wingi wao"

Mfalme wa Moabu akawaambia wazee wa Midiani

Wamobau na Wamidiani walikuwa watu wa makundi mawili tofauti, lakini Wamidiani walikuwa wanishi kwenye nchi ya Moabu wakati ule.

Huu umati utakula kila kitu tulicho nacho kama vile maksai walavyo nyasi za kondoni

Jinsi Waisraeli watavyowaangamiza maadui zao kumeongolewa kama vile makaisai wanavyokula nyasi za kondeni

Sasa Balaki mwana wa Zippori alikuwa mfalme wa Moabu

Huu ndio wasifu wa Balaki katika habari hii

Numbers 22:5

Akatuma wajumbe

"Balaki akatuma wajumbe"

Beori

Hili ni jina la baba wa Balaam.

Pethori

Hili ni jina la mji

katika nchi ya taifa lake na watu wake

"wa taifa la Balaam na watu wake"

Akamwita

"Balaki akamwita Balaam."

Wanafunika uso wa dunia

"walikuwa wengi sana"

uso wa dunia

Hii inamaanisha sehemu ya juu ya dunia

kuwafukuza

"kuwaondosha"

Najua kuwa yeyote unayembariki hubarikiwa na yeyote unayemlaani atalaaniwa

"Najua unazo nguvu za kubariki na kulaani watu"

Numbers 22:7

malipo ya uganga

"Pesa ya kumlipa Balaamu ili awalaani Waisraeli"

Wakafiaka kwa Blaamu

"Walienda kwa Balaamu"

Wakamwambia maneno ya Balaki

"maneno" inamaanishaujumbe wa Balaki. "Wakamwambia ujumbe toka kwa Balaki"

nitawaletea

"Nitawaambia"

Numbers 22:9

Mungu akaja kwa Balaamu

"Mungu akaonenkana kwa Balaamu"

Ni akina nani hawa waliokuja kwako?

"Niambie juu ya watu hawa waliokuja kwako"

Tazama hawa watu ... kuwafukuza.

Tazama 22:5

Kuwafukuza

"kuwaondosha"

Numbers 22:12

kwa sababu wamwbarikiwa

"Kwa sababu Nimewabariki"

Numbers 22:15

Wakaja kwa Balaamu

"Walienda kwa Balaamu"

watu hawa

"kundi hili la watu"

Numbers 22:18

Hata kama Balaki atanipa ikulu yake ikiwa imejaa fedha

Balaamu anasisitiza kuwa hakuna kitakachomfanya avunje utii wake kwa BWANA

sitaweza kufanya dhidi ya maneno ya BWANA... na kufanya pungufuau zaidi ya kile anachoniambia.

Inamaanishsa kuwa Balaamu hataacha kumtii BWANA kwa namna yeyote.

Numbers 22:21

akatandika punda wake

akamwanadaa punda wake tayari kwa safari

hasira za Mungu zikawaka

"Munga akajawa na hasira"

kama adui wa Balaamu

"ili aweze kumzuia Balaamu"

akiwa na upanga mkononi

"akiwa na upanga tayari kwa kushambulia

yule punda akageuka na kwenda shambani

"Yule punda alifanya hivi ili kumwepuka malaika wa BWANA"

ili arudi barabarani

"kumrudisha"

Numbers 22:24

Akasongea zaidi ukutani

Alifanya hivi ili kumwepuka malaika wa BWANA barabarani

Akasogea

"punda alisogea"

na kuubana mguu wa Balaalmu ukutani

"akaukandamiza mguu wa Balaamu na kumwumiza Balaamu"

Numbers 22:26

Hasira za Balaamu zikawaka

Tazama 22

Numbers 22:28

Kisha BWANA akafungua kinywa cha Punda na akaongea

"Kisaha BWANA akampa punda uwezo wa kuongea kama vile binadamu awezavyo kuongea"

Akamwabia Balaamu

"Yule punda akamwambia Balaamu"

Je, mimi si punda wako ambaye umenipanda maishani mwako mwote mpaka hivi sasa?

"Mimi ni punda wako ambaye umenipanda maishani mwako mwote, mpka hivi sasa."

Je, nimewahi kuwa na tabia ya kukufanyia hivi hapo awali?

"sijawahi kuwa na tabia ya kukufanyia hivi"

Numbers 22:31

Basi BWANA akafungua macho ya Balaamu, na akamwona malaika wa BWANA

"Kisha BWANA akampa Baalamu uwezo wa kumwonamalaika wa BWANA"

akiwa na upanga mkononi mwake

Tazama 22:21

Balaamu akainamisha kichwa chake chini

Balaamu akajinyenyekeza

Kwa nini umempiga punda wako mara tatu

"usingempiga punda wako mara tatu

kama adui yako

"ili kukupinga"

Kama asingekuwa amegeuka kutoka kwangu... ningekuwa nimekuua na yeye kumwacha hai

punda alimwokoa Balaamu

Numbers 22:34

kwa hiyo sasa, kama haikupendezi

"kwa hiyo kama hutaki mimi niendelee"

kwa hiyo Balaamu akaendelea na wale viongozi

Tazama 22:2

Numbers 22:36

Amoni

Tazama 21:12

Je, mimi sikutuma watu kukuita?

"Kwa hakika nilituma watu kukuita"

Kwa nini hukuja kwangu

"ulipaswa kuja kwangu"

Je, mimi sina uwezo wa kukufanya uheshimiwe?

"kwa hakika unajua kuwa mimi ninauwezo wa kukulipa pesa kwa ajili ya ujio wako kwangu"

Numbers 22:38

Je, mimi sina mamlaka ya kusema chochote

"Lakini sinsa mamlaka yakusema chochote ninachotaka"

maneno ambayo Mungu ameweka kinywani mwangu

"ujumbe ambao Mungu ananitaka niuseme"

Kiriathi Huzothi

Haya ni mjina ya miji

baadhi ya hiyo nyama

"baadhi ya hiyo nyama kutoka kwenye ile sadaka"

Numbers 22:41

mpaka mahali pa juu pa Baali

Tazama 21:19

Numbers 23

Numbers 23:1

Balaki

Tazama 22:2

Uandae mafahri saba na kondoo dume saba

"uchinje mafahari saba na kondoo dume saba kuwa sadaka"

simama kwenye sadaka yako ya kuteketezwa na mimi nitaenda

"baki hapa na sadaka yako ya kuteketetezwa na mimi nitaenda umbali kidogo"

Numbers 23:4

nimetoa sadaka ya fahari na kondoo dume

"Nimechinja fahari nakondoo dume na kuwateketeza kama sadak"

BWANA akaweka ujumbe kwenye kinywa cha Balaamu

"BWANA akamwambia Balaamu kile alichotaka akamwambie Balaki"

Numbers 23:7

Balaki amenileta kutoka Shamu ... mfalme wa Moabu kutoka katika milima ya mashariki,

Virai hivi vinamaanisha kitu kilekile

Njoo, unilaanie Yakobo kwa ajili yangu; ... njoo umtie unajisi Israeli;

Virai vyote vinamaanishsa kitu kilekile vimetumika kuongeza msisitizo kwamba Balaki alitaka Balaamu kulaani Israeli.

Nawezaje kuwalaani wale ambaoMungu hajawalaani? Nawezaje kuwapinga wwale ambao Mungu hawapingi?

"Lakini siwezi kuwalaani wale ambao Mungu hajawalaani. Siwezi kuwapinga wale ambao Mungu hajawapinga"

Numbers 23:9

Kwa muwa kutoka juu ya miamba ninamwaona ... kutoka juu ya milima ninamtazama

Virai hivi viwili vinamaanishakitu kimoja. "Balaamu alimwona Israeli kutokea juu ya mlima."

Ninamwona ... ninamtazama

Kiwakilishi cha "mwo" na "m" kinawakilisha Waisraeli.

Kuna watu

"Kuna kundi la watu"

na hawajioni wenyewe kama ni taifa la kwaida

"wanajiona wenyewe kuwa taifa maalumu"

Numbers 23:10

Nani awezaye kuyahesabu mavumbi ya Yakobo au hata kuhesabu robo ya Israeli?

"Hawa Waisraeli ni wengi mno kuwahesabu. Hakuna awezaye kuwahesabu hata robo kwa sababu ni wengi mno"

kifo cha mtu mwenye haki

"kifo cha amani cha mtu mwenye haki"

mtu mwenye haki ... uwe kama wake

Hizi ni semi zinazowaongelea Waisraeli kuwa kama mtu mmoja.

Numbers 23:11

Balaki

Tazama 22:2

Umenifanyia nini?

"Siwezi kuamini ulichonifanyia!"

lakini ona

Hii inaonesha matukio ya kutisha yanayofuata

Kwa nini nisiwe mwangalifu kusema kile ambacho BWANA ameweka kinywani mwangu?

Lazima niwe mwangalifu kusema kile ambacho BWANA ananiambia kusema."

ameweka kinywani mwangu

Tazama 22:38

Numbers 23:13

Huko sasa unaweza kunilaania hawa watu

"Huko utanilaania Waisraeli"

Shamba la Zofimu

Neno "Zofimu" linamaanisha 'kutazama' au 'kupelelza'

Mlima Pisiga

Tazama 21:19

Numbers 23:16

na kumwekea ujumbe kinywani mwake

Tazama 22:38

Akasema

"Kisha BWANA akaksema"

Balaki, na usikilize ... Nisikilize mimi wewe mwana wa Zippori

Sentensi hizi zinamaanisha kitu kilekile na zimetumika kusisitiza umuhimu wa Balaki kuwa msikivu.

mwana wa Zippori

Tazama 22:2

Numbers 23:19

Je,alishawahi kuahidi kitu pasipo kukitekeleza? Je, alishawahi kusema kuwa atafanyakitu bila kufanya?

"Hajawahi kuahidi kitu pasipo kutimiza kile alichoahidi. Amekuwa akifanya kama alivyosema kuwa atafanya."

Nimeamuriwa kubariki

"Mungu ameniamuru kuwabariki Waisraeli"

Numbers 23:21

magumu katika Yeriko ... tabu katika Israeli

Virai hivi vinamaana moja ambayo yaweza kuwa 1) Mungu amempatia Israeli mambo mazuri tu 2) Hakuna dhdambi katika Israeli ambayo itamfanya awahukumu.

kelele za wafalme wao ziko pamoja nao

"Wanapiga kelele kwa furaha kwa sababu BWANA ni mfalme wao"

kwa nguvu kama za nyati

Mfano huu unamaanisha kuwa nguvu za BWANA ni sawa na nguvu za nyati

Numbers 23:23

Hakuna uganga utakaofanyika dhidi ya Yakobo ... hakuna uchawiutakaomwumiza Israeli

Virai hivi vinamaanisha kitu kilekile kwamba; hakuna laana ambayo mtu yeyote ataifanya katika taifa la Israaeli itakayofanikiwa.

Itasemwa

"watu watasema"

Tazama kile ambacho Mungu amefanya

"Yatazame mambo mazuri ambayo Mungu amewafanyia!"

Numbers 23:24

watu wanainuka kama simba jike ... na kunywa damu ya windo lake

Israeli wanavyowaangamiza maadui ni kama simba anavyoshambulia windo lake.

Numbers 23:25

Balaki

Tazama 22:2

Sijakuambia kuwa nitasema yote ambayo BWANA ananiambia kusema?

"Nilikuambia mapema kuwa nitasema yote ambayo BWANA ananiambia kusema."

Numbers 23:28

ambalo ambalo unalitazama chini lile jangwa

"ambalo unalitazama lile jangwa ambapo Waisraeli walikuwapo"

Numbers 24

Numbers 24:1

kama hapo awali

"kama alivyofanya nyakatiza nyuma"

Numbers 24:2

Akayainua macho yake

"akatazama juu"

Roho wa Mungu akamjia

Roho wa Muungu alimtawala wakati wa kutoa unabii.

Akapokea huu unabii

"Mungu alimpatia huu unabii"

Balaamu mwana wa Beori

Tazama 22:5

ambaye macho yake yamefunuliwa

anaona na kuelewa

Numbers 24:4

Taarifa kwa ujumla

Balaamu anaendelea kutoa unabii kwa kuwezeshwa na Mungu

Huongeae ... Huona ... humwinamia

Haya ni maneno ya Balaamu

humwinamia

Hili ni tendo la heshima

macho yake yakiwa yamefumbuliwa

"macho yakiwa yamefumbuliwa" inamaaniaha kuwa Balaamu alikuwa amepokea uwezo wa kufahamu kile ambacho Mungu alimtaka aseme.

Jinsi zilivyo nzuri hema zako, ewe Yakobo, mahali unapoishi, Israeli

Virai hivi vyote vina maana moja na vinaonesha jinsi kambi za Waisraeli zilivyokuwa nzuri kwa Balaamu.

Numbers 24:6

Taarifa kwa ujumla

Balaamu anaendelea kutabiri kwa uwezo wa Mungu

Wamesambaa kama bonde

Balaamu anawaongelea Waisraeli kuwa walikuwa wengi kiasi cha kulijaza bonde lote

kama bustani zilizo pembezonimwa mto

Balaamu anawaongelea Waisraeli kama bustani iliyomwagiliwa maji na itoayo mavuno menegi.

kama miti ya mishubiri iliyopandwa na Mungu

"Mishubiri ambayo BWANA ameipanda"

kama mfano wa mierezi pembezoni mwa maji

Mierezi ilikuwa miti mierfu sana huko Israeli. Balaamu anawaongelea Waisraeli kama mierezi iliyokuwa sana na kuwa miti mikubwa kwa sababu ya maji mengi.

Numbers 24:7

Taarifa kwa ujumla

Balaamu anaendelea kutabiri kwa uwezo wa Mungu.

Maji yanatirika ... zimemwagiwa maji

"Mungu ataibariki Israeli kwa maji mengi kwa ajili ya mazao"

mbegu zao zimemwagiwa maji vizuri

"Watakuwa na maji mengi kwa ajili ya mbegu zao ili kusitawisha mazao"

Mfalme wao atakuwa juu ... na ufame wao utaheshimiwa

Sentensi hizi zinamaanisha kitu kimoja zinasisitiza kuwa Mungu atawabariki ukilinganisha na mataifa mengine.

Mfalme wao atakuwa juu ya Agagi

Neno "juu" linamaanishsa heshima ya juu na mamlaka kuliko Agagi.

Ufalme wao utaheshimiwa

"watu wengine watauheshimu ufalme"

Numbers 24:8

Taarifa kwa ujumla

Balaamu anaendelea kutabiri kwa uwezo wa Mungu.

Mungu anamtoa

Mungu anawaleta Waisraeli

na nguvu kama za nyati

Waisraeli watakuwa na nguvu

Atawameza mataifa

Watawaangamiza maadui wao

Numbers 24:9

Taarifa kwa ujumla

Balaamu anamaliza kutoa unabii kwa uwezo wa Roho wa Mungu

Ananyatia kama siimba mume, na kama simba jike.

Inamaanisha kuwa wako tayari kushambulia.

Nani anayejaribu kumshambulia

"Hakuna anayethubutu kumsumbua"

Kila mmoja anayembarki na abarikiwe; na kila mmoja anayemlaani na alaaniwe

"Mungu awabariki wale wanawabariki Waisraeli; na awalaani wale wanowalaani Wasraeli"

Numbers 24:10

Hasira za Balaki zikawaka

"Balaki alijawa na hasira"

akaipiga mikono yake kwa pamoja

Hii ilikuwa ishara kubwa ya kuchanganyikiwa na hasira

Numbers 24:12

Hata kama Balaki atanipatia ikulu yake ikiwa imejaa fedha na dhahabu

"Inaonesha kuwa hakuna kitu ambacho kitamfanya Balaamu kumkaidi Mungu

Je, sikuwaambia haya?

"Niliwaambia haya."

watu hawa

"Waisraeli"

Numbers 24:15

Balaamu mwana wa Beori

Tazama 22:5

ambaye macho yake yamefumbuliwa

Tazama 24:2

aliye na maaarifa toka kwake yeye aliye juu

"Anayejua vitu ambavyo Mungu aliye juu ameyafunua"

humpigia magoti

Hii ni ishara ya kujitoa kwa Mungu

Numbers 24:17

Taarifa kwa ujumla

Balaamu anaendelea na unabii wake wa kwanza

Ninamwona, lakini hayuko karibu sasa. Ninamtazama, lakini siyo karibu

Virai hivi vinamaanisha kitu kimoja. Hapa Balaamu anatoa maona ya tukio la wakati ujao. Kiwakilishi "mwo" kinamaanisha kiongozi wa Israeli wa baadaye.

Nyota itatokea katika Yakobo

"Nyota" inaonesha mfalme wa Waisraeli ambaye atainuka katika mamlaka.

Katika Yakobo

"kutoka katika uzao wa Yakobo"

Na fimboya enzi itainuka katika Israeli

Neno "fimbo" linamaanisha mfalme mwenye mamlaka

Katika Israeli

Kutoka kwa Waisraeli hapo baadaye"

atawapigapiga viongozi wa Moabu

Yaweza kumaanisha 1) atavunja vichwa vya viongozi wa Moabu 2) atawaharibu viongozi wa Moabu.

uzao wa Sethi

Hii inamaanisha Wamoabu, waliokuwa uzao wa Sethi

Numbers 24:18

Taarifa kwa ujumla

Balaamu anamaliza unabii wake wa kwanza kati ya nabii nne alizotoa.

Edomu atakapokuwa miliki ya Israeli

"Waisraeli wataimilki Edomu"

Na Seiri pia itakuwa milki yao

"Israeli atawaangamiza watu wa Seiri"

Kutoka kwa Yakobo atatoka mfalme

"Yakobo" ni kiwakilishi cha watu wote wa Isreli

katika mji

"mji wa Ari ambao Balaki alikutana na Balaamu"

Numbers 24:20

Balamu akamtazama Amaleki

Amaleki inamaanisha watu wa Amaleki ambao pia aliwatolea unabii.

mwisho wake utakuwa

amametumia iwakilishi "wake" kwa sababu ametumia kiwakilishi cha mtu mmoja.

Numbers 24:21

Wakeni

Hili ni jina la kundi la watu walitokana na Kaini

Mahali unapoishi pana usalamu

"Mahali unapoishi panalindwa"

na viota vyake viko kwenye miamba

"mahali penu pana usalama kama vile kioyta kilivyo salama kinapokuwa kwenye miamba"

Lakini pamoja na hayo, Kaini ataharibiwa na Ashuru atakapowachukua mateka."

"Lakini Waashuru watawaharibu Wakeni na kuwachukua kama mateka"

Numbers 24:23

Ole wake atakayesalia Mungu atakapoyafanya haya?

"Hakuna atakayesalia Mungu atakayefanya haya"

Kittimu

Hili ni jina la mji katika kisiwa kilicho katika bahari ya kati.

wao pia wataishia katika uharibifu

"Mungu atawaharibu pia"

Numbers 25

Numbers 25:1

Shittimu

Hili ni jina la mahali kule Moabu

kuisujudia

"hili ni tendo la ibaada"

Peori

Tazama 23:28

Hasira ya BWANA ikawaka

Tazama 21:19

Numbers 25:4

viongozi wote wa watu

"viongozi wote wa watu ambao wana hatia ya kuabudu sanamu"

ili waonekane wakati wa mchana

Viongozi wa Waisraeli watawaua watu hawa na kuacha maiti zao nje ili watu wote wawaone

Viongozi wa Israeli

"Kwa viongozi wa Israeli wasiokuwa na hatia ya kuabudu sanamu"

Numbers 25:6

akaleta mwanake mmoja aliyekuwa miongoni mwa familia yake

"akaleta mwanamke wa Kimidiani kwenye kambi ya Waisraeli ili alale naye"

mbele ya macho ya Musa na watu wa Israeli

"mbele ya macho ya" ni nahau inayomaanisha walisikia juu yao, au walipata taarifa juu yao"

Eliezeri

Tazama 3:1

Numbers 25:8

Akamfuata

"Finehasi akamfuata"

Numbers 25:10

ameigeuza hasira yangu isiwe kwa wana wa Israeli

"Amesababisha mimi nisiwe na hasira juu ya wana wa Israeli"

sijawaangamiza watu wa Israeli kwa hasira yangu

"Sijawaangamiza wana wa Israeli kwa hasira yaku kali"

Numbers 25:12

Kwa hiyo waambie, 'BWANA anasema, "Tazama, ninampa Finehasi agano langu la amani ... watu wa Israeli."

"Kwa hiyo mwambie Finehasi kuwa nitampatia ... wana wa Israeli."

Numbers 25:14

Sasa

Hii inatutoa kwenye habari nyingine na kutupeleka kwenye habari ya Zimri na Cozibi.

alyeuawa

"ambaye Finehasi alimwua"

Zimri ... Salu ... Zuri

Haya ni majina ya wanaume

Cozibi

Hili ni jina la mwanamke

Numbers 25:16

kwa kuwadanganya

"kwa kukudanganya wewe"

waliwaongoza katika uovu

"Waliwashawishi ninyi kufanya uovu huu"

swala la Peori ... kwa swala la Peori

Virai hivi vinamaanisha kuwa vitu hivi vyote vilitokea pale Peori.

Peori

Tazama 23:28

amabye aliuawa

"ambaye Finehasi alimwua"

Numbers 26

Numbers 26:1

Wahesabu watu wote

"Wahesabu wanaume wote katika jamii"

miaka ishirini na zaidi

"umri wa miaka 20 nazaidi"

Numbers 26:3

wakawaambia

"wakawaambia viongozi wa Waisraeli"

Uwanda

Uwanda ni eneo tambarare

miaka ishirini na zaidi

"umri wa miaka 20 na zaidi"

Numbers 26:5

Taarifa kwa ujumla

Viongozi wa Israeli wanawahesabu wanaume wenye umri wa miaka 20 na zaidi, kwa kufuata makabila yao na familia zao.

ndiye aliyekuwa mzaliwa wa kwanza wa Israeli

"Israeli" inamaanisha Yakobo

kutoka kwa mwana wake

Neno "wake" inamaanisha Reubeni

Numbers 26:8

Taarifa kwa ujumla

Tazama 26:5

Eliabu ... Dathani ... Abiramu

Tazama 16:1

Numbers 26:10

Dunia ilifungua kinywa na kuwameza pamoja

"BWANA ndiye aliyesababishaardhi ifunguke, n a wale wanaume wakaangukia shimoni"

moto uliteketeza wanaume 250

"BWANA alisababisha moto uwaue wanaume 250"

uzao wa Kora

"familia yote ya Kora

kufa

"mwisho"

Numbers 26:12

Taarifa kwa ujumla

Tazama 26:5

Numbers 26:15

Taarifa kwa ujumla

Tazama 26:5

Numbers 26:19

Taarifa kwa ujumla

Tazama 26:5

Numbers 26:23

Taarifa kwa ujumla

Tazama 26:5

Numbers 26:26

Taarifa kwa ujumla

Tazama 26:5

Numbers 26:28

Taarifa kwa ujumla

Tazzama 26:5

Numbers 26:30

Taarifa kwa ujumla

Tazama 26:5

Numbers 26:33

Taarifa kwa ujumla

Tazama 26:5

Numbers 26:35

Taarifa kwa umumla

Tazama 26:5

Huu ndio uzao wa Yusufu

"Hawa walikuwa wazao wa Yusufu, wazao wa wana wakeambao ni Manase na Efraiimu"

uliohesabiwa toka kila koo

"waliwahesabu kutoka katika kila ukoo wao"

Numbers 26:38

Taarifa kwa ujumla

Tazzama 26:5

Numbers 26:42

Taarifa kwa ujumla

Tazama 26:5

Numbers 26:44

Taarifa kwa ujumla

Tazama 26:5

Numbers 26:48

Taarifa kwa ujumla

Tazama 26:5

Numbers 26:51

jumla kuu

"jumla"

601,730

Laki sita, elfu moja, mia sab na thelathini.

Numbers 26:52

Ile ardhi itagawanywa

"mtaigawa ardhi"

wanaume hawa

Tazama26:5

Kwa kufuata idadi ya majina yao

"kwa idadi ya watu katika kila ukoo"

Numbers 26:54

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kuongea na Musa

utawagawia urithi mkubwa

"utawapa ardhi zaidi kuwa urithi"

waliohesabiwa

"ambao viongozi wa Israeli waliwahesabu

ardhi itagawiwa

"mtaigawa ardhi"

kwa kupigiwa kura

"kwa kupiga kura"

utagawiwa

"utaigawa"

watagawiwa

"na mtaigawa ardhi kwao"

Numbers 26:57

Taarifa kwa ujumla

Hii ni orodha ya ukoo wa Lawi. Musa aliwahesabu Walwi kwa namna tofauti na makabila mengine kwa sababu hawakupokea ardhi yeyote.

Zilizohesabiwa kwa kufuata ukoo

"ambao viongozi waliwahesabu kwa kufuata ukoo"

Gerishoni ... Kohathi ... Merari ... Amramu

Tazama 3:17

Alimzalia Amramu watoto wao

"Yeye na Amramu walikuwa na watoto"

Numbers 26:60

Nadabu ... Abihu ... Ithamari

Tazama 3:1

Walipotoa sadaka kwa BWANA sadaka ya moto isiyokubalika

Tazama 3:3

waliohesabiwa

"ambao viongozi waliwahesabu"

Elfu ishirini na tatu

"23,000"

Umri wa mwezi mmoja na zaidi

"umri wamwezi mmoja na kuendelea"

hawakuhesabiwa

"lakini viongozi hawakuwahesabu"

hawakupewa urithi

"kwa sababu BWANA alisemawasipewe ardhi kama uriti wao"

Numbers 26:63

walihesabiwa na Musa na Eliezeri yule kuhani

"ambao Musa na Eliezeri waliwahesabu"

aliyehesabiwa na Musa na Haruni

"Ambaye Musa na Haruni waliwahesabu"

wana wa uzao wa Israeli walipohesabiwa

"walipowahesabu wana wa uzao wa Israeli"

Numbers 26:65

Hapakuwa na mtu aliyebaki, isipokuwa

"watu pekee waliokuwa walikuwa"

mwana wa Yefune

Tazam 13:5

mwana wa Nuni

Tazama 11:28

Numbers 27

Numbers 27:1

Kisha wakaja kwa Musa binti wa Zelofehadi ... wamana wa Yusufu

"Hawa ni mabinti wa uzao wa Zerofehadi waliomjia Musa"

Zelofehadi, mwana wa Hefa ... Mahlahi. Noha, Hogla, Milika, na Tiriza

Tazama 26:33

Gileadi ... Machiri

Tazama 26:28

Numbers 27:2

Walisimama

"Binti wa Zelofehadi walisimama"

Waliompinga BWANA katika lile kundi ka Kora

"Waliokufa kwa sababu walikuwa miongoni mwa wafuasi waliompinga BWANA"

kwa dhambi zake

"kwa sababu ya dhambi zake"

Numbers 27:4

Kwa nini jina la baba yetu liondolewe miongoni mwa ukoo wa jamaa za zake kwa sababu ya kukosa wana?

"Usiliondoe jina la baba yetu katika ukoo kwa sababu hakuwa na mwana"

Tupeni ardhi miongoni mwa ndugu wa baba zetu

"Tupeni ardhi kule ambako ndugu wa baba zetu wanaishi"

Numbers 27:6

miongoni mwa ndugu za baba zake

"mahali ambako ndugu za baba zake wanaishi"

Numbers 27:9

Taarifa kwa ujumla

Hii inaendeleza sheria za Mungu juu ya nani anapaswa kupokea ardhi kama mtu hakuwa na wana.

Hii itakuwa sheria iliyoanzishwa kwa amri kwa ajil ya watu wa Israeli

"Itakuwa sheria ambayo watu wote wa Israeli wataitii"

alivyoniamuru

kiwakilishi "ni" kinamaanisha Musa

Numbers 27:12

Milima ya Abarimu

Hii ni safu ya milima huko Moabu

ambayo nimewapa wana wa Israeli

ambayo nitawapa wana wa Israeli

pia lazima ukusanyike na watu wako

"lazima ufe"

Kama Haruni kaka yako

"kama Haruni kaka yako mkubwa"

ninyi wawili mlipinga amri yangu

"Hii inamaanisha Musa na Haruni"

Katika jangwa la Sini

Tazama 13:21

Pale ambapo maji yalitoka kwenye mwamba, katika hasira yako

Hii inamaanisha lile tukio ambalo Mungu alitengeneza maji kwa muujiza yakatoka kwenye mwamba. Mungu alimwambia Musa auambie mwamba, lakini badala yakae Musa akaupiga kwa sababu alikuwa na hasira dhidi ya watu

ulishindwa kuniheshimu mimi kama mtakatifu

"haukunichukulia kama mtakatifu"

mbele ya macho ya watu wote

"mbele ya kundi lote"

maji ya Meriba

Tazama 20:12

Numbers 27:15

Mungu wa wote wenye mwili

"Mungu awapaye wanadamu pumzi"

mtu awe juu ya watu

"mtu wa kuwaongoza watu"

mtu ambaye atatoka na kuingia kuja kwao na kuwatoa kisha kuwarudisha

mtu ambaye atawaongoza watu wote na kuongoza jeshi katika vita

ili kwamba watu wako wasije kuwa kama kondoo wasiokuwa na mchungaji

Hii inamaanisha kuwa watu wasipokuwa na kiongozi watazungukazunguka

Numbers 27:18

Mchukue Joshua mwana wa Nuni, mtu ambaye Roho yangu hukaa

Roho ya BWANA yumo ndani ya Joshua, Hii inamaanisha kuwa Joshua humtii BWANA na kufuata amri zake.

umwekee mikono yako juu yake

"umwekee mikon yako juu yake ili umwagize"

umwamuru kuwaongoza mbele ya macho yao

"na mbele yao umwamuru Joshua kuwaongoza watu wa Israeli"

Numbers 27:20

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kuongeea na Musa juu ya Joshua

Utaweka baadhi ya mamlaka yako kwake

"utampa baadhi ya mamlaka yako"

Urimu

Hili lilikuwa jiwe la thamani ambalo kuhani mkuu alilivaa kifuani pake. Alilitumia kwa kutambua mapenzi ya Mungu.

Yeye pamoja na watu wa Israeli, ambao ni watu wote

"Wote yeye na taifa lote la Israeli"

Numbers 27:22

na kumweka mbele ya

"na akamwambia kusimama mbele ya"

Akaweka mikono yake juu yake na kumwamuru aongoze

kiwakilishi "a" kinamaanisha Musa, na kiwakilishi "ku" kinamwakilisha Joshua.

Akaweka mikono yake yake

Kitendo cha kuweka mikono ilikuwa njia ya kumweka mtu wakfu ili afanye kazi maalumu ya Mungu.

aongoze

"kuwa kiongozi wa Waisraeli"

kama BWANA alivyokuwa amemwamuru kufanya

kiwakilishi "mu" kinamwakilisha Musa

Numbers 28

Numbers 28:1

kwa wakati uliopangwa

"kwa wakati ambao nimeuchagua"

chakulacha sadaka yangu kilichotengenezwa kwa moto ili kutoa

"chakula cha sadaka ambacho mtaiteketeza kwenye madhabahu"

kutoa harufu nzuri kwa ajili yangu

"harufu ninayoifurahia"

Numbers 28:3

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kumwambia Musa kile ambacho watu wanatakiwa kufanya.

sadaka iliyotengenezwa kwa moto

"sadaka ya kuteketezwa"

iliyochanganywa na

"ambayo mmeichanganya na"

sehemu ya kumi ya efa

"lita 2"

robo ya hini

"lita moja"

mafuta yaliyokamuliwa

"mafuta safi ya mizeituni yaliyokamuliwa"

Numbers 28:6

ilyoamriwa mlima Sayuni

ambayo BWANA aliamuru pale mlima Sayuni

iliyotengenezwa kwa moto

uliyoiteketeza kwa moto kwenye madhabahu

robo ya hini

"lita moja"

utaimimina mahali patakatifu hiyo sadaka ya kinywaji kwa BWANA

"Lazima iwe sadaka, ya kinywaji n a lazima uimimine mahali patkatifu kwa ajili ya BWANA"

Alivyotolewa

"kama yule mliyemtoa"

Numbers 28:9

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kumwambia Musa kile ambacho watu wanapaswa kufanya

sehemu ya kumi mbili ya efa

"takribani lita 4.5"

iliyochanganywa na mafuta

"ambayo mmeichanganya na mafuta"

na ile sadaka ya kinywaji

"ile sadaka ya kinywaji inayoambatana nayo"

Numbers 28:11

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kumwambia Musa kile ambacho watu wanapaswa kufanya

sehemu ya kumi tatu

"lita sita"

sehemu za kumi mbili

"takribani lita 4.5"

sehemu ya kumi ya efa

"lita 2"

ilyochanganywa na mafuta

"ambayo mmeichanganya na mafuta"

iliyotengenezwa kwa moto

ambayo mmeiteketeza madhabahuni

Numbers 28:14

nusu ya hini

"lita 2"

sehemu ya tatu ta hini

"lita 1.2"

robo ya hini

"lita moja"

beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kwa BWANA.

"Lazima mtatoa beberu mmoja kwa BWANA kuwa sadaka ya dhambi"

Numbers 28:16

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kumwambia Musa kile ambacho watu wanapaswa kufanya

siku ya kumi na nne, ya mwezi wa kwanza ... katika siku ya kumi na tano ya mwezi

siku ya 14, ya mwezi wa 1, ... siku ya 15 ya mwezi huu, "Hii inamaanisha mwezi wa kwanza wa kalenda ya Kiyahudi"

itakuwa Pasaka ya BWANA

"mtasherehekea Pasaka ya BWANA"

kutakuwa na sikukuu

"mtakuwa nasikukuu"

Mtakula mikate isiyokuwa na chachu

mtakula mikate isiyotiwa chachu

siku ya kwanza

siku ya 1

kutakuwa na kusanyiko takatifu l a kumheshimu BWANA

"Mtakusanyika pamja kumwabudu na kumheshimu BWANA." Kirai cha kusanyiko takatifu kinamaanishsa kuwa watu wanakusanyika kumwabudu BWANA. Kumwabudu BWANA ni kusanyiko takatifu.

Numbers 28:19

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kumwambia Musa kile ambacho watu wanapaswa kufanya

mtatoa sadaka iliyotengenezwa kwa moto

mtateketeza sadaka madhabahuni

sehemu za tatu za efa

"lita sita"

iliyochanganywa na mafuta

"ambayo umeichanganya na mafuta"

sehemu za pili

takribani lita 4.5

sehemu ya kumi ya efa

"lita 2"

kufanya upatanisho

"kupatana"

Numbers 28:23

inayotakiwa kila asubuhi

"ambayo BWANA huitaka kila asubuhi"

kama ilivyofafanuliwa hapa

"kama Mimi, BWANA ilkivyofafanua hapa"

kile chakula cha sadaka kilichotengenezwa kwa moto

"mtateketeza chakula cha sadaka madhabahuni"

kuwa harufunzuri kwa BWANA

"kama harufu nzuri kwa BWANA"

hiki kitatolewa kuwa sadaka

"mtakitoa"

mtakuwa na kusanyiko takatifu ili kumheshimu BWANA

"Mkusanyike pamoja kumwabudu na kumheshimu BWANA:

Numbers 28:26

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kumwambia Musa kile ambacho watu wanatakiwa kufanya

sikuya malimbuko

"Hii ni siku ya sikukuu ambayo wanatoa sadaka ya unga kwa BWANA.

Mtakuwa na kusanyiko takatifu la kumwabudu BWANA

"Mtakusanyika pamoja kumwabudu na kumheshimu BWANA"

uliochanganywa na mafuta

ambao mmeuchanganya na mafuta

sehemu za kumi tatu za efa

"lita 6"

sehemu za kumi tatu za efa

"lita 6"

sehemu za kumi mbili

"Takribani lita 4.5"

Numbers 28:29

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kumwambia Musa kile ambacho watu wanatakiwa kufanya

sehemu ya kumi moja

"lita 2"

unga mwembamba uliochanganywa na mfuta

unga mwembamba ambao mmeuchanganya na mafuta

kufanya upatanisho

"kupatana"

sadaka zake za vinywaji

sadaka za vinywaji vinavyoambatana nayo

Numbers 29

Numbers 29:1

Taarifa kwa uumla

BWANA anaendelea kumwambia Musa kile ambacho watu wanatakiwa kufanya

siku ya kwanza ya mwezi wa saba

"siku ya 1, ya mwezi wa 7 ya mwezi, katika kalenda ya Kihebrania"

mtakuwa na kusanyiko takatifu la kumwabudu BWANA

"Kusanyikeni pamoja ili kumwabudu na kumheshimu BWANA"

Itakuwa siku ya kupiga matarumbeta

"Itakuwa siku ambayo makuhani watapiga matarumbeta"

Numbers 29:2

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kumwambia Musa kile ambacho watu wanatakiwa kufanya

Numbers 29:3

sadaka ya unga

sadaka ya unga inayotolewa pamoja navyo

uliochanganywa na mafuta

"ambao mmeuchanganya na mafuta"

shsmu ya kumi tatu ta efa

"lita 6"

sehemu ya kumi mbili

"lita4.5"

sehemu ya kumi

"lita 2"

ili kufanya upatanisho

"kupatana"

Numbers 29:6

katika mwezi wa saba ... mwanzo wa kila mwezi

"mwezi wa 7 ...mwanzo wa kila mwezi katka kalenda ya Kihebrania."

kilka mwezi ... pamoja na sadaka maalumu ... na sadaka zake

"kwa kila mwezi, sadaka maalumu za kuteketezwa ... pamoja nazo"

sadaka za kuteketezwa za kila siku, sadaka zake za unga na sadaka zake za vinywaji.

"sadaka za kila siku za kuteketezwa pamoja na sadaka za unga na sadaka za vinywaji zinazoambatana nazo"

utakuwa ukitii kilichoamriwa

"utatii amri za BWANA"

sadaka iliyotengenezwa kwa moto

sadaka uliyoteketeza madhabahuni kwa BWANA"

Numbers 29:7

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kumwambia Musa kile ambacho watu wanatakiwa kufanya

siku ya kumi ya mwezi wa saba

"siku ya 10 ya mwezi wa 7 kwa kalenda ya Kihebrania.

mtakuwa na kusanyiko takatifu

kusanyikeni ili kumwabudu na kumheshimu BWANA"

Numbers 29:9

uliochanganywa na mafuta

"ambao mmeuchanganya na mafuta"

sehemu ya kumi tatu

lita 6

sehemu ya kumi mbili

lita 4.5

sehemu ya kumi ya efa

lita 2

ya upatanisho

inayopatanisha

pamoja na sadaka za unga na sadaka zake za vinywaji

"pamoja na sadaka za unga na sadaka za vinywaji zinazoambatana nazo"

Numbers 29:12

Taarifa kwa uumla

BWANA anaendelea kumwambia Musa kile ambacho watu wanatakiwa kufanya

siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba

"siku ya 15, ya mwezi wa 7, ya kalenda ya Kihebrania"

mtakuwa na kusanyiko takatifu

"kusanyikeni ili kumwabudu na kumheshimu BWANA"

mtazitunza hizo sikukuu kwa ajili ya BWANA.

"Mtazikumbuka hizo sikukuu kwa ajili ya BWANA"

sadaka iliyotengenezwa kwa moto

"mtaiteketeza kwenye madhabahu"

mafahari wachanga kumi na tatu, kondoo waume wawili, na wanakondoo waume kumi na nne

mafahari wachanga 13, kondoo waume 2, na wanakondoo waume 14.

Numbers 29:14

uliochanganywa na mafuta

"ambao umeuchanganya na mafuta"

sehemu ya kumi tatu ta efa

lita 6

mafahari kumi na tatu ... wanakondoo waume kumi na nne

mafahari 13, wanakondoo 14

sehemu a kumi mbili

lita 4.5

sehemu ya kumi ya efa

lita 2

sadaka yake ya unga, na sdaka ya vinywaji

sadaka ya unga na sadaka ya vinywaji inyoambatana na sadaka ya kila siku ya kuteketezwa,

Numbers 29:17

siku ya pil ya kusanyiko

"siku ya 2 ya sikukuu." neno "kusanyiko" linamaanisha sikukuu za majuma.

fahari wachanga kumi na mbili, kondoo waume wawili, na wanakondoo waume kumi na nne

"fahari 12, kondoo waume 2, na wanakondoo waume14."

kama ilivyoamriwa

"kama BWANA alivyoamuru"

sadaka yake ya unga na sadaka yake ya vinywaji

"pamoja na sadaka yake yaunga na sadaka yake ya vinywaji inayoamabatana nayo"

Numbers 29:20

siku ya tatu ya kusanyiko

"siku ya 3 ya sikukuu. Neno "kusanyiko" linamaanisha sikukuu ya majuma

mafahari kumi na moja, kondoo dume wawili, na wanakondoo waume kumi na nne

"mafahari 11, kondoo waume 2, na wanakondoo waume 14."

kama ilivyoamriwa

"kama BWANA alivyoamuru"

sadaka zakeza unga, na sadaka zaka za vinywaji

"pamoja na sadaka zake za unga na sadaka zake za vinywaji zinazoambatana nazo."

Numbers 29:23

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kumwambia Musa kile ambacho watu wanatakiwa kufanya wakati wa sikukuu za mwezi wa saba.

siku ya nne ya kusanyiko

"siku ya 4 ya sikukuu." neno "kusanyiko" linamaanisha sikukuu za majuma.

wanakondoo wa kiume kumi na nne

"wanakondoo wa kiume 14"

kama ilivyoamriwa

"kama BWANA alivyoamuru"

sadaka zake za unga, na sadakazakae za vinywaji

"pamoja na sadaka zake za unga, na sadaka zake za vinywaji zinazoambatana nazo."

Numbers 29:26

siku ya tano ya kusanyiko

"siku ya 5 ya sikukuu." Neno kusanyiko linamaanisha sikukuu za majuma."

wanakondoo waume kumi na nne

"wanakondoo waume 14"

kama ilivyoamriwa

"Kama BWANA alivyoamuru"

sadaka zake za unga, na za vinywaji

"pamoja na sadaka zake za unga na za vinywaji zinazozambatana nazo."

Numbers 29:29

siku ya sita ya kusanyiko

"siku ya sita ya sikukuu." Neno kusanyiko linamaanisha sikukuu za majuma."

wanakondoo waume kumi na nne

"wanakondoo waume 14."

kama ilivyoamriwa

"kama BWANA alivyoamuru"

sadaka zake za unga, na sadaka zake za vinywaji

"pamoja nasdaka zake za unga, na sadaka zake za vimywaji zinazoambatana nazo."

Numbers 29:32

siku ya saba ya kusanyiko

"sikuy a7 ya kusanyiko." Neno "kusanyiko" linamaanisha sikukuu za majuma."

wanakndoo waume kumi na nne

"wanakondoo waume 14"

kama ilivyoamriwa

"kama BWANA alivyoamru"

sadaka zake za unga, na sadaka zake za vinywaji

"pamoja nasadaka zake za unga na sadaka zake za vinywaji zinazoambatana nazo"

Numbers 29:35

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kumwambia Musa kile ambacho watu wanatakiwa kufanya wakati wa sikukuu za mwezi wa saba.

siku ya nane

siku ya 8

mtakuwa na kusanyikok lingine makini

"kutaneni tena ili kumwabudu BWANA sawa na kusanyiko la siku ya kwanza "

Sadakailiyotengenezwa kwa moto

"mtaiteketeza kwenye madhabahu"

Numbers 29:37

sadaka zake za unga na sadaka zake za vinywaji

"sadaka za unga na sadaka za vinywaji"

kama ilivyoamriwa

"kama BWANA alivyoamuru"

zadakazake za unga, na sadaka zake za vinywaji

"pamoja nasadaka zake za uunga , na sadaka zake za vinywaji zinazoambatana nazo"

Numbers 29:39

Hivi ndivyo utakavyotoa

"Hizi sadaka ndizo utakazotoa"

sikukuu za kila mwaka

"sikukuu zilizopangwa"

Numbers 30

Numbers 30:1

Mtu yeyote atakayefanya nadhiri, au kuapa kwa kiapo

Virai hivi viinamaanisha kitu kilekile. Vimetumika kuonesha unuhimu wa kiapo.

ili kufunga nafsi yake

"kujitoa ili kutimiza kiapo" au "kuahidi kufanya kitu fulani"

asivunje neno lake. HeAtafanya sawa na ahadi yake imtokayo kinywani mwake

"Lazima atimize ahadi yake"

asivunje neno lake

Lazima atimize ahadi zake"

sawa na ahadi yake imtokayo kinywani mwake

"atafanya kila kitu anachosema kuwa atakifanya"

Numbers 30:3

na kufunga nafsi yake kwa kiapo

"anajitoa mwenyewe ili kutimiza ahadi" au "ahadi ya kufanya jambo fulani"

nadahari na ahadi

maneno haya yana maana moja "Nadhriri"

na kufunga nafsi yake

"ambacho ameahidi mwenyewe kukitimiza"

kumzuia

"kuahirisha alichoahidi"

ndipo nadhiri zake zitakuwa naguvu. kila ahadi ... itabaki kuwa naguvu.

"atatakiwa kutimiza kile alichoahidi"

Numbers 30:5

nadhiri yake na ahadi yake

"nadhiri yake"

alizofanya

"ambazo alijitoa kufanya" au "zile alizofanya"

zitabaki kuwa nguvu

tazama 30:3

Numbers 30:6

ahadi zake makini ambazo ametumia kufunga nafsi yake

"ahadi zake makini ambazo amejitoa mwenyewe kuzitimiza"

na kama atazitengua

"kama atazitengua ahadi zake"

hazitakuwa na nguvu

"hatalazikmika kuzitimiza"

BWANA atamsamehe

"BWANA atamsamaehe kwa kutotimiza ahadi zake"

angali katika hivyo viapo

"wakati bado amejitoa kutimiza viapo hivyo"

bila kufikiri

"kitu kilichofanywa pasipo kufikiri"

katika hivyo viapo

"vitu ambavyo mwenyee amehadi kuvifanya"

Numbers 30:8

kiapo alichofanya ... manenoya midomo yake ya bila kufikiri

sentensi hizi zinamaanisha kitu kilekile. Kirai cha pili kinafafanua kiapo ambacho yule mwanamke alifanya.

maneno ya midomo yake ya bila kufikiri

"Maneno aliyosema pasipo kufikiri" au "ahadi za bila kufikiri"

ambayo kwayo amefunga nafsi yake

"ambayo amejitoa mwenyewe kutimiza"

BWANA atamfungua

"BWANA atamsamehe"

Numbers 30:9

Taarifa kwa ujumla

Musa anaenedelea kuwaeleza vingozi wa makabila ambacho BWANA ameamuru

mwanamke aliyetalikiwa

"mwanamke aliyepewa talaka na mwanamume"

ambacho atakisema kufunga nafsi yake

"ambacho amejitoa mwenyewe kutimiza"

kitabaki na nguvu kinyume na yeye

Tazama 30:3

kama m mwanamke atafanya kiapo katika nyumba ya mume wake

"kama mwanamke aliyeolewa atafanya nadhiri"

basi viapo vyake vitasimama ... vitabaki na nguvu

Tazama 30:3

viapo vyakae vitasimama ... na vifungo alivyovifanya vitabaki na nguvu

"basi viapo vyake na ahadi zake ... vitabaki na nguvu"

Numbers 30:12

basi chochote ambacho kitatoka katika kinywa chake

"basi chochote atakachosema"

Havitakuwa na nguvu

Tazama 30:6

BWANA atamfungua

"BWANA atamsamehe kwa kutotimiza viapo vyake"

Numbers 30:13

Kila kiapo ambacho ... kinaweza kuthibitika au kubatilishwa na mume wake

"Mume wa yule mwanamke anaweza kuthibitisha au kubatilisha kiapo chochote alichofanya ambacho kinamfunga ili kujikana"

kinachomfunga

"ambacho ameahadi kukifanya"

ahadi zake zinazomfunga

"ahadi"

kwa sababu hakusema chochote wakati alipozisikia

"kwa sababu hakumwambia chochote juu ya ahadi hizo"

Numbers 30:15

basi ataajibika kwa dhambi zake

"kama hatatimiza ahadi zake, hatakuwa na hatia ya dhambi zake, na badala yake mawanamume atakuwa na hatia badala yake"

Numbers 31

Numbers 31:1

Uwalipizie kisasi Wamidiani kwa kile walichowafanyia Waisraeli

BWANA alikuwa anawaadhibu Wamidiani kwa sababu waliwashawishi kuabudu masanamu

utakufa na kukusanyika nawatu wako

Ni tafsida ya Musa kufa n a roho yake kwenda kule ambako mababu zake waliko

Numbers 31:3

andaeni baadhi ya majeshi yenu kwa ajili ya vita

"Wapatie silaha baadhi ya wanaume"

wakawapige Wamidiani na kubeba kisasi cha BWANA

"Nenda upigane na Wamidiani na muwadhibu kwa ajili ya kile walichotutendea"

elfu moja ...elfu kumi na mbili

"1,000 ... 12,000"

maelefu elfu wa Israeli na nawanaume elfu

"wanaume wengi wa Israeli"

wanaume elfu kumi na mbili

makabila 12 walituma wanaume, pamoja na kabila la Lawi. Kila kabila lilituma wanaume 1,000 vitani"

wanaume elfu moja walitolewa kwa kila kabila kwa ajili ya vita

"kila kabila lilitoa wanaume 1,000 kwa ajili ya vita"

Numbers 31:6

Evi, Rekemu, Zuri, Huri, na Reba

Haya ni majinaya wafalme wa Midiani

Balaamu mwana wa Beori

Tazama 22:5

Numbers 31:9

likachukua mataeka

"walichukua vitu vya Wamidiani na kuvifanya kuwa vyao"

Walichoma moto miji yao yote walimoishi na kambi zao zote

"Jeshi la Waisraeli walichoma moto miji yote ambamo Wamidiani waliishi na kambi zote za Wamidiani"

Numbers 31:11

Walichukua

"Jeshi la Israeli lilichukua"

Miliki

Hii inamaanishsa vile vitu walivyochukua baada ya kuwaua Wamidiani

uwanda

eneo kubwa tambarare

Numbers 31:13

majemadari wa maelfu

Hawa ni viongozi wa majeshi waliongoza wanaume zaidi ya 1,000 lakini pungufu ya wanaume 10,000.

wa maelfu ... maakida wa mamia

"maelfu ya maaskaari ... maaskari mamia"

maakida wa mamia

hawa ni viongozi wa majeshi walioongoza zaidi ya wanaume 1000 lkaini pungufu ya wanaume 1000.

Je, mmewaachca wanawake wote kuishi?

Jeshi lilivunja sheria kwa kuwaacha hai wanawake na watoto. Musa aliwakemea wanajeshi.

Numbers 31:16

Tazama

Hii ilikuwa ni kuwataka wasikilize na kuelewa ambacho msemaji alikuwa anawaambia wasikilizaji

aliyelala na mwanaume

aliyefanya ngono na mwanaume

Numbers 31:18

Taarifa kwa uumla

Musa anawaambia majemedari wa jeshi la Waisraeli juu ya kujitakasa mbele za BWANA.

ambao hawajalala na mwanaume

mabikra

Ninyi wote

Yeyote ambaye alipigana kwenye hivyo vita, si majemedari tu.

mtajitakasa wenyewe

Lazima wawesafi kiroho kabla hawajarudi kambini.

Kilichotengenezwa kwa ngozi za wanyama na manyoya ya mbuzi, na kila kitu kilichotengenezwa kwa mbao

"kila kitu ambacho mtu alitengeneza kwa kutumia ngozi za wanyama, manyoya ya mbuzi, au mbao"

Numbers 31:21

Taarifa kwa ujumla

Eliezeri anawafundisha maaskari taratibu za kujitakasa mbele ya BWANA baada ya kwenda vitani

Dhahabu, fedha, shaba,vyuma, bati, risasi

Hivi ni vyuma ambavyo vilikuwa vinatumika wakati ule

haviwezi kupita kwenye moto

"ambavyo haviwezi kuungua"

mtakiweka katika moto

"viwekeni motoni"

maji ya takaso

Tazama 19:17

ndipo mtakapokuwa safi

Huu ndio utaraibu wa kuwa safi mbele ya BWANA

Numbers 31:25

vihesabu vitu vyote vilivyochukuliwa nyara

"vihesabu vitu vyote ambavyo maaskari wa wamevichukua"

Nyara

Hivi ni vitu vilivyochukuliwa na maaskari

viongozi wa watu kufuata ukoo

"vioingozi wa kila ukoo"

Numbers 31:28

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kuongea na Musa

Taarifa kwsa ujumla

"kwangu" inamaanisha BWANA

Kisha toza kodi ambayo itatolewa kwangu kutoka kwa wanajeshi waliokuwa wameenda vitani

"kusanya kodi kutoka kwenye nyara za wanajeshi na uzitoe kangu."

kati ya mia tano

"kila 500"

kutoka katika nusu yao

"kutoka katika nusu ya maaskari"

itakayotolewa kwangu

"ambavyo atavitoa kwangu"

Numbers 31:30

Taarifa ka ujumla

BWANA anaendelea kuongea na Musa

Pia kutoka katika nusu ya Waisraeli

"Pia kutoka katika nusu ya nyara za Waisrael."

kati ya hamsini

"kila 50"

wanaotumika

wale wanaosimamia masikani na sadaka kwa BWANA

Numbers 31:32

Sasa

Neno hili limetumika hapa ili kuonesha mwisho wa habari hii kuu. Pia Musa anaanza kusikiliza juu ya kiasi cha nyara na kiasi gani kilitolewa kwa maaskari, kwa watu, na kwa BWANA.

maksai elfu sabini na mbili, punda elfu sitina na moja, na wanawake elfu thelathini na mbili

"makisai 72,000, punda 61,000, na wanawake 32,000."

amabao walikuwa hawajalala na mwanaume

mabikra

Numbers 31:36

Taarifa kwa ujumla

Musa anaorodhesha nyara ambazo zitaenda kwa maasikari na kodi itakayoenda kwa BWANA.

ile nusu iliyokuwa imetunzwa kwa ajiai ya maaskari

"sehemu ya kondoo wa maaskari"

elfu thelathini na sita

36,000

sabaini na mbili

72

Numbers 31:39

Taarifa kwa ujumla

Musa anaorodhesha nyara ambazo zitaenda kwa maasikari na kodi itakayoenda kwa BWANA.

sitini na moja

61

elfu kumi na sita

16,000

thelathini na mbili

32

ilitakiwa kuwekwa sadaka ya BWANA

"kuwa sadaka ya BWANA"

Numbers 31:42

tarifa kwa ujumla

Musa anaorodhesha nyara ambazo zitaenda kwa maasikari na kodi itakayoenda kwa BWANA.

makisai elfu thelathini n a sita

makisai 36,000

wanawake elfu kumi na sita

wanawake 16,000

Numbers 31:47

Taarifa kwa ujumla

Musa anaorodhesha nyara ambazo zitaenda kwa maasikari na kodi itakayoenda kwa BWANA.

Taarifa kwa ujumla

Ile kodi ya sehemu ya watu iliuwa juu kodi ya maaskari

Numbers 31:48

majemedari wa maelfu

Tazama 31:13

juu ya maelfu ... juuya mamia

"maaskari zaidi ya maelfu ... maskari zaidi ya mamia"

Makaptateni wa mamia

Tazama 31:13

watumishi wako wamewahesabu

"watumishiwako." Hii ni njiaya kujinyenyekeza wakati wa kuongea na mtu mwenye mamlaka makubwa.

hakuna hata mmoja wao aliyekosa

"tunajua kwa uhakika kuwa kila mmoja yuko hapa"

Numbers 31:50

Taarifa kwa ujumla

Maofisa wa jeshi wanaendelea kuongea na Musa.

metali, timbi, pete za mhuri, vipini na kikuku

Hivi vyote ni vitu vya mapambo ambavyo watu huvaa.

ili kujifanyia upatanisho kwa BWANA

"kumshukuru Mungu kwa kutuokoa maisha yetu"

dhahabu na vitu vyote vilivyotengenezwa kwa ufundi

"vitu vyote vya dhahabu"

Numbers 31:52

vitu vyote vya dhahabu ... kutoka kwa mamia vilikuwa na uzito ...

"dhahabu yote ambayo makamanda wa jeshi walitoa kwa BWANA ilikuwa na uzani wa"

16,750

"mia saba na hamsini"

shsekeli

shekeli 1 ni sawa na garamu 11

kama ukumbusho wa watu wa Israeli kwa BWANA

dhahabu itawakumbusha watu kuwa BWANA aliwapa ushindi, Pia itamkumbusha BWANA kuwa watu walitimiza kisasi kwa Wamidiani.

Numbers 32

Numbers 32:1

Sasa

Hili neno "sasa" linatumika hapa kuonesha mwanzo wa habari mpya. Musa anaanza kueleza historia ya Kabila la Reubeni na Gadi.

Atarothi, Diboni, Jazeri, Nimrahi, Heshiboni, Elealehi, Sabamu, Nebo na Beoni

Haya ni majina ya miji

Numbers 32:4

Taarifa kwa ujumla

Watu kutoka kwa Reubeni na Gadi wanaendelea kuongea na Musa, Eliezeri, na viongozi wengine

Haya ni maeneno ambayo BWANA laichukua mbele ya watu wa Israeli

"ardhi ambayo BWANA ametuwezesha kuwaangamiza watu waishio ndani yake"

Sisi watumishi wako

watu wa Reubeni na Gadi wantumia lugha hii kuonesha unyenyekevu wao kwa mtu mwenye mamlaka ya juu.

kama tumepata kibali mbele ya macho yako

"kama tumepata kibali kwako" au "kamaumependezwa na sisi"

tunaomba ardhi hii tupewe

"utupe ardhi hii"

Usituvushe ng'ambo ya Yorodani

"Usituvushe ng'ambo ya Yorodani ili kupata umiliki wa ardhi kule"

Numbers 32:6

Je. mngependa ndugu zenu waende vitani wakati ninyi mkikaa hapa?

"Si sahihi kwenu kukaa hapa wakati ndugu zenu wanaenda vitani"

Kwa nini kuwafisha moyo wana .... kwenye nchi ambayo BWANA amewapa?

"Msikatishe tamaa mioyo ... ardhi ambayo BWANA amewapa"

kuwafisha moyo wa Israeli wasivuke

"kuwafisha moyo watu wa Israel ili wasivuke" "au "msiwasababishe watu wa Israeli ili wasitake kuvuka kwenda"

Numbers 32:8

Taarifa kwa ujumla

Musa anaendelea kuongea na watu wa Reubeni na Gadi

Bonde la Eskoli

Tazama 13:23

Waliiona ile ardhi

"Waliwaona wale watu hodari na ile miji katika hiyo ardhi"

wakawafisha moyo watu wa Israeli

Tazama 32:6

Numbers 32:10

hasira ya BWANA iliwaka

"BWANA akakasirika sana"

hakuna mtu

"hakuna mtu kati ya watu." Kirai hiki kinamaanishsa watu wote waume kwa wake

walionifuata kwa ukamilifu

"walinitii kwa ukamilifu"

Yefune ... Nuni

Haya ni majina ya wanaume

Mkenizi

Hili ni jina la kikundi cha watu

Numbers 32:13

Hasira za BWANA ziliwaka

"BWANA alikasirika sana

miaka arobaini

"miaka 40"

kile kizazi ... kilipoteketea

"kizazi chote ... macho yake kilipokufa"

kilichofanya maovu mbele za macho yake

"kilichofanya maovu mbele za macho ya BWANA"

mmetokea katika nafasi za baba zenu

"mmeanza kutenda kama babu zenu"

ili kuongeza hasira ya BWANA kwa Israeli

"kumfanya BWANA kuwa na hasira zaidi kwa Israeli"

watu hawa wote

"kizazi chote hiki cha watu"

Numbers 32:16

tutajipanga kijeshi

"tutakuwa tayari tukiwa na silaha" au "tutakuwa tayari kupigana vitani"

kwenye miji ya maboma

"katika miji salama"

Numbers 32:18

Taarifa kwa ujumla

Viongozi wa Reubeni na Gadi wanaendelea kuongea

apate urithi

"amechukua urithi wake wa ardhi"

Numbers 32:20

kama mtajipanga wenyewe

"kama mtachukua silaha zenu"

Mbele ya BWANA

"katika uwepo wa BWANA"

mpaka atakapowafukuza maadui zake

"mpaka BWANA atakapowawezesha maaskari kuwaangamiza maadui na kuwafu"kuza kutoka katika uwepo wake

na nchi itawaliwe na Israeli

"na katika uwepo wake Waisraeli watawatawala watu wanaoishi katika nchi hiyo"

mtaweza kurudi

"mtaweza kurudi katika nchi hii katika upande wa mashariki wa Yorodani

Hamtakuwa na hatia mbele za BWANA na mbele ya Israeli

Inamaanisha 1) "mtakuwa mmekamilisha wajibu wenu kwa BWANA na kwa Israeli 2)"Hakutakuwa nalawama toka kwa BWANA au kwa Israeli"

Numbers 32:23

Mwe na hakika kuwadhambi yenu itaonekana

"Mjue kwa uhakika kuwa BWANA atawaadhibu kwa dhambi yenu"

watumishi wako

"hii ni namna ya kunyeyekea pale mtu anapoongea na mtu mwenye mamlaka ya juu"

Numbers 32:26

tutavuka

"tutavuka mto Yorodani"

kila mtu ambaye yuko tayari kwa vita

"kila mtu aliyejiandaa kwa vita"

Numbers 32:28

kila mwanamume anayetakiwa kuwa vitani

"kila mwanamume aliyetayari akiwa na siilaha yake"

kama nchi mtaitawala mbele zenu

"kama BWANA atawatawala mbele yenu hao watu wanaoishi katika nchi hiyo"

basi mtawapa urithi wao katika nchi ya Kanaani"

Basi kile kizazi cha Gadi na Reubeni watapokea ardhi pamoja nanyi kule Kanaani

Numbers 32:31

Tutavuka tukiwa na silaha zetu

"Tutavuka Yorodani tukiwa tayari kwa vita"

urithi wetu

"Sehemu ya ardhi ambayo tutaridhi"

utabaki upande huu

"utakuwa wetu"

Numbers 32:33

ufalme wa Sihoni ... na wa Ogu

"ufalme wa Sihoni ... na ufalme wa Ogu"

Numbers 32:34

Diboni, Aroeri ...

Haya ni majina ya miji

Numbers 32:37

Heshiboni, Elealehi ...

Haya ni majina ya miji.

baadaye waliyabadili majina yao

"baadaye watu walibadili majina ya miji hii"

Numbers 32:40

Jairi ... Nobaha

Haya ni majina ya wanaume

Havothi Jairi ... Kenathi

Haya ni majina ya miji

Numbers 33

Numbers 33:1

pamoja na makundi y ao ya kijeshi

Tazama 1:1

kama ilivyoamriwa na BWANA

"kama BWANA alivyoamuru"

kutoka kwao kulivyokuwa kwa kila walipotoka

"kutoka eneo moja hadi jingine"

Numbers 33:3

Taarifa kwa ujumla

Musa anaorodhesha maeneo ambayo Waisraeli walipita baada ya kutoka Msri.

mwezi wa kwanza, waliondoka siku ya kumi na tano

Huu ni mwezi wa kwanza wa kalenda ya Kihebrania

Wana wa Israeli waliondoka waziwazi mbele ya macho ya Wamisri

"Waisraeli waliondoka wakati Wamisri wakiwaona"

wazaliwa wao wa kwanza

"wazaliwa wao wa kwanza wa kiume"

ka kuwa pia alikuwa ameiadhibu miungu yao

"kwa kuwa pia alikuwa amedhihirisha kuwa yeye ni mkuu kulikko miungu yao"

Numbers 33:5

Taarifa kwa ujumla

Musa anaorodhesha maeneo ambayoaWaisraeli walipita walipotoka Misri.

walisafiri kutoka

"waliondokda"

mwisho wa nyika

"kwenye mpaka wa jangwa

Numbers 33:8

Taarifa kwa ujumla

Musa anaorodhesha maeneo ambayoaWaisraeli walipita walipotoka Misri.

na kupita katikati ya bahari

Hii inamaanisha BWANA alipoigawa habari ya shamu ili kwamba Waisraeli waweza kutoroka toka jeshi la Wamisiri

chemichemi kumi na mbilu ... na mti sabin ya mitende

chemichemi 12 ... na mti 70 ya mitende

Numbers 33:11

Taarifa kwa ujumla

Musa anaorodhesha maeneo ambayoaWaisraeli walipita walipotoka Misri.

ambapo watu walikoswa maji ya kunywa

" "ambapo watu hawakupata maji ya kunywa"

Numbers 33:15

Taarifa kwa ujumla

Musa anaorodhesha maeneo ambayoaWaisraeli walipita walipotoka Misri.

Numbers 33:19

Taarifa kwa ujumla

Musa anaorodhesha maeneo ambayoaWaisraeli walipita walipotoka Misri.

Numbers 33:23

Taarifa kwa ujumla

Musa anaorodhesha maeneo ambayoaWaisraeli walipita walipotoka Misri.

Numbers 33:27

Taarifa kwa ujumla

Musa anaorodhesha maeneo ambayoaWaisraeli walipita walipotoka Misri.

Numbers 33:31

Taarifa kwa ujumla

Musa anaorodhesha maeneo ambayoaWaisraeli walipita walipotoka Misri.

Numbers 33:35

Taarifa kwa ujumla

Musa anaorodhesha maeneo ambayoaWaisraeli walipita walipotoka Misri.

Numbers 33:38

mwaka wa araobaini baada ...

"baada ya miaka 40"

katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano

siku ya 1 y a mwezi wa 5 kwa kalenda ya Kihebrania.

Numbers 33:40

Wakaanani, mfalme wa Aradi

"Mkanaani mfalme wa Aradi"

Aradi

Hili lilikuwa jinala nji wa Kanaani.

walisikia juu ya ujio wa Israeli

"walisikia kuwa wana wa Israeli walikuwa wanakuja"

Numbers 33:41

Taarfa kwa ujumla

Musa anaorodhesha maeneo ambayoaWaisraeli walipita walipotoka Misri.

Numbers 33:44

Taarifa kwa uumla

Musa anaorodhesha maeneo ambayoaWaisraeli walipita walipotoka Misri.

Numbers 33:47

Taarifa kwa ujumla

Musa anaorodhesha maeneo ambayoaWaisraeli walipita walipotoka Misri.

Nyanda

eneo kubwa lililotambarare

Numbers 33:50

na kuharibu mahali pao pote plipoinuka

"kuvunja mahali pao pote palipoinuka"

Numbers 33:53

Taarifa kwa uumla

BWANA anaendelea kumwambia Musa kile ambacho watu wanapaswa kufanya.

Mtairithi ardhi

Madai ya Waisraeli ya kuwa ile aradhi ni yao ndiko kunakofanya kusema kuwa watairithi ile ardhi.

Kura itakapoanguka kwenye kila ukoo, hiyo ardhiitakuwa mali yake

"Kila ukoo utapata ardhi kulingana na kura itakavyokuwa"

Numbers 33:55

Tarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kumwambia Musa kile ambacho watu wanapaswa kufanya.

kama siindano machoni mwenu na miibakatika mbavu zenu

kama vile kitu idogo sana kinavyosababisha jicho kuuma ndivyo itakavyokuwa kwa Iwaisraeli kama watamwacha Mkanaani kukaa katika ile nchi.

Numbers 34

Numbers 34:1

jangwa l a Sini

Tazama 33:1

Numbers 34:4

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kumwambia Musa ile Mipaka ilipo ya nchi ambayo BWANA anawaptia Waisraeli.

Numbers 34:6

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kumwambia Musa ile Mipaka ilipo ya nchi ambayo BWANA anawaptia Waisraeli.

Numbers 34:7

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kumwambia Musa ile Mipaka ilipo ya nchi ambayo BWANA anawaptia Waisraeli.

Mlima Hori

Tazama 20:22

Numbers 34:10

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kumwambia Musa ile Mipaka ilipo ya nchi ambayo BWANA anawaptia Waisraeli.

Numbers 34:13

kwa makabila tisa na nusu

Hii inamaanisha kuwsa yale makabila yanayobaki ambayo tataishi ule upande wa magharibi wa Mto Yorodani katika nchi ya Kanaani. Tle makabila ya Reubeni na Gadi na nusu ya Manase yamepata urithi wao upande wa Mashariki wa Mto Yorodani.

kufuata jinsi walivyopewa urithi kwa jamaa ya kabila yao

"Kwa kufuata jinsi BWANA alivyoigawa mali kwa makabila ya mababu

Yale makabila mawili na nusu

"Kabila la Reubeni la Gdi, na nusu ya Manase"

Numbers 34:16

Taarifa kwa ujumla

Hii ndiyo orodha ya wanaume watakaosaidia kuigawa ardhi kati ya yale makabila

Numbers 34:19

Taarifa kwa ujumla

Hii ndiyo orodha ya wanaume watakaosaidia kuigawa ardhi kati ya yale makabila

Numbers 34:21

Taarifa kwa ujumla

Hii ndiyo orodha ya wanaume watakaosaidia kuigawa ardhi kati ya yale makabila

Numbers 34:24

Taarifa kwa ujumla

Hii ndiyo orodha ya wanaume watakaosaidia kuigawa ardhi kati ya yale makabila

Numbers 34:27

Taarifa kwa ujumla

Hii ndiyo orodha ya wanaume watakaosaidia kuigawa ardhi kati ya yale makabila

Numbers 35

Numbers 35:1

nyanda

eneo kubwa ambalo ni tambarare

wa ardhi yao kwa Walawi

BWANA hakuwapatia Walawi ardhi yao, kwa hiyo walitakiwa kuishi kwenye miji ambayo ilikuwa ya makabila mengine.

eneo la malisho

eneo la malisho ambalo mifugo kuchungiwa

Numbers 35:3

dhiraa elfu moja

"mita 457"

Numbers 35:5

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kumwambia Musa kile ambacho watu wanapaswa kufanya.

dhiraa elfu mbili

dhiraa moja ni sawa na sentimita 46

Numbers 35:6

kama mtu ameua mtu

Hii inawahusu watu walioua. Lakini bado haijaamuliwa kama waliua kwa makusdi.

arobaini na mbili ... arobaaini na nane

"42 ... 48"

Numbers 35:8

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kumwambia Musa kile ambacho watu wanapaswa kufanya.

Numbers 35:9

pasipo kukusudia

"kwa bahati mbaya"

Numbers 35:12

mlipa kisasi

mtu anayetaka kulipa kisasi kwa kumwua mtuhumiwa

ili kwamba mtuhumiwa asije akauawa bila kwanza kusikilizwa na jamii

"ili kwamba mtu yeyote asije akamwua mtuhumiwa kabla jamii haijamhukumu barazani"

Numbers 35:14

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kumwambia Musa kile ambacho watu wanapaswa ufanya.

Numbers 35:16

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kumwambia Musa kile ambacho watu wanapaswa ufanya.

kwa hakika huyo anatakiwa kuuawa

"Lazima mwue"

Numbers 35:19

Mwenye kulipa kisasi cha damu

"Mtu yule ambaye anamlipizia mwuaji"

atamshinda mtu yeyoteyule anayemchukia

"atamzidi nguvu mtu fulani" au "amemtendea kwa ujeuri mtu fulani"

yule mtuhumiwa aliyempiga hakika atauawa

"mtuhumia lazima auawe"

Numbers 35:22

bila kukusudia

"bila kupanga kutokana na chuki hapa awali"

bila kumvizia

"bila kukusudia kujaribu kumwumiza"

Numbers 35:24

mlipa kisasi

Tazama 35:19

watu watamwokoa mtuhumiwa

jamiiitatakiwa kuamua kuwa kile kifo hakikusudiwa.

ambaye alipakwa mafuta matakatifu

ambaye mlimpaka mafuta matakatifu"

Numbers 35:26

mlipa kisasi

Tazama 35:19

Numbers 35:29

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kumwambia Musa kile ambacho watu wanapaswa ufanya.

kwa kizazi chote

"na uzao wenu utakaoisi baada yenu"

mwuaji atauawa

"mtu fulani lazima amwua mwuaji"

kama neno la ushahidi litatolewa

kulingana n a ushahidi wa mashahidi"

Lakiniushahidi wa mtu mmoja unaweza usitoshe kusababisha mtu kuuawa

"Lakini neno l s mshahidi mmoja tu hautoshi kumfanya mtu auawe"

Numbers 35:31

kwa hakika lazima auawe

"Lazima mwue"

Msimruhusu ... kurudi kwenye mali zake

M"simruhusu ... kuondoka kwenye ule mji wa ukimbizi nakurudi nyumbani kuishi kwenye mali zake"

kwa namna yeyote

"kwa kupokea fidia"

Numbers 35:33

Msiiharibu nchi mnayokaa kwa namna hii, kwa kuwa damu ya mwuaji huharibu nchi.

Msiifanye nchi ile mnapoishi isikubalike kwangu kwa namna hii, kwa sababu damu ya mwuaji huifanye nchi isikubalike kwangu"

kwa namna hii

kwa kutokutii sheria inayohusiana na mtu anayeua mtu"

Hakuna sadaka ya upatanisho inayoweza kufanywa kwa nchi pale damu inapomwagika juu yake isipokuwa kwa damu ya mtu aliyeimwaga.

"mtu anapokuwa amemwaga damu kwenye nchi, ni adhabu ya kifo cha mwuaji tu ndiyo inayoweza kufanyika kuwa fidia kwenye nchi hiyo"

Numbers 36

Numbers 36:1

Machiri

Tazama 26:28

BWANA alikuamuru

"BWANA alikuamuru"

Zelofehadi

Tazama 26:33

Numbers 36:3

utaondolewa kutoka kwenye mgao wa mababu zao

"kamwe hatutakuwa kwenye mgao wa Mababu zetu"

Utaongezwa

"Utakuwa mali ya"

utaondolewa kwenye mgao uliopangwa kwenye urithi wetu.

"Kamwe hautakuwa sehemu ya urithi wetu"

mwaka wa yubilee ya wana wa Israeli

Hi ni sherehe inayotokea mara moja kila baada ya miaka hamsini. Katika sherehe hii, ardhi yote iliyouzwa lazima arudishiwe mmiliki wake wa kwanza.

mgao wao utaunganishwa

"mgao wao utakuwa mali ya..."

mgao wao utaondolewa kwenye mgao wa mababu zao

"watachukua mgao wa ardhi wa kabila letu"

Numbers 36:5

kwa neno l a BWANA

"kutokana na kile alichosema BWANA"

Acha waolewe na wale ambao wao wanafikiri ni vizuri

"Acha waolewe na wale wanaowataka"

lakini lazima waolewe ndani ya kabila ya baba yao

"lakini ni laziima waolewe na mtu kutoka kwenye kabila la baba yao"

Numbers 36:7

Hakuna mgao

Hakuna sehemu ya ardhi"

Numbers 36:8

aliye na mgao kwenye kabila lake

"aliye na mgao wa ardhi kwenye kabila lake"

aweze kuwa na urithi

ardhi ambayo kila ukoo unaimiliki inaongolewa kama urithi waliopokea.

Hakuna mgao utakaobadilika kutoka kabila nyingine

"hakuna anayeweza kuhamisha umiliki wa mgao wowote wa ardhi kutoka kabila moja hadi nyingine"

Numbers 36:10

Mahilaha, Tiriza, Hogila, Milika, na Noha

Tazama 26:33

urithi wao

"ardhi ile waliyopewa kama urithi"

Numbers 36:13

Nyanda

eneo kubwa amabalo ni tambarare

Deuteronomy 1

Deuteronomy 1:1

zaidi ya Yordani

Hii urejea kwa nchi kuvuka mto wa Yordani, mashariki mwa Israel. Musa alikuwa mashariki mwa Yordani wakati alipozungumza na wanaIsraeli.

Sufu...Parani...Tofeli...Labani...Hazarothi...DiZahabu

Haya ni majina ya sehemu.

Ni safari ya siku kumi na moja kutoka Horebu... kwenda Kadeshi ya Barnea.

"Huchukua siku kumi na moja kutembea kutoka Horebu...kwenda Kadeshi ya Barnea"

Kumi na moja

11

Deuteronomy 1:3

Ilitokea katika mwaka wa arobaini, katika mwezi wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi, ambayo Musa alizungumza.

"Walikuwa wameishi jangwani miaka 40, miezi 11, na 1 siku, wakati Musa alipozungumza"

Arobaini

40th

katika mwezi wa kumi na moja, katika siku ya kwanza ya mwezi.

Huu ni mwezi wa kumi na moja wa Kiabrania. Siku ya kwanza iko karibu katikati mwa mwezi Januari kwa kalenda za Magharibi.

kumi na moja

11th

Yahwe alikuwa amevamia

"Yahwe alikuwa amewawezesha wanaisraeli kushinda"

Sihon...Og

Haya ni majina ya wafalme.

Heshbon... Ashtarothi ya Edrei

Haya ni majina ya miji

Deuteronomy 1:5

Zaidi ya Yordani

Hii urejea kwa nchi kuvuka mto wa Yordani, mashariki mwa Israeli. Musa alikuwa mashariki mwa Yordani aliposema hivi.

kuzunguma nasi

Neno "nasi" urejea kwa Musa na watu wengine wa Israel.

Umeishi muda wa kutosha katika nchi ya mlima

Hii ni nahau. "Hauhitaji kukaa karibu na mlima zaidi tenda.

Deuteronomy 1:7

Taarifa ya jumla

Musa anaendelea kuwakumbusha watu wa Israeli kile alichosema Yahwe kwao.

Geuka na anza safari yako

"Anza tena safari yako"

nchi ya mlima...Euphrates

Yahwe anaeleza maeneo katika nchi kwamba ameahidi kuwapa wanaisraeli.

nchi ya mlima

Hili ni eneo katika milima karibu na eneo ambapo Wamorites waliishi.

nchi ya chini

eneo la nchi ambayo liko chini na tambarare

Tazama

"Zingatia yale ninayoenda kusema"

Nimeweka nchi mbele yako

"Sasa naenda kukupa nchi hii"

kwamba Yahwe aliapa

Yahwe anazungumza kama alikuwa mtu mwingine.

baba

Neno "baba" ni neno lenye maana sawa na mababu.

Deuteronomy 1:9

Taarifa ya jumla

Musa aliendelea kuwakumbusha watu wa Israeli ambayo Yahwe alivyosema nao.

Niliongea nanyi kwa watkia huo

Hapa "Ni" urejea kwa Musa. Maneno "kwa wakati huo" urejea kwa wakati wanaisrael walipokuwa Horebu, ambayo ni sawa kama mlima Sinai.

Siwezi kuwabeba mimi peke yangu

Hapa "kuwabeba" umaanisha "kuwaongoza ninyi" au kuwatawala ninyi." "Hii ni zaidi kwangu kuwaongoza mwenyewe"

kama umati wa nyota za mbinguni

Hii ni kutia chumvi ambako kunamaanisha Mungu ameongeza idadi ya wanaisraeli

mara elfu

Maneno "mara elfu" ni fumbo la "nyingi sana"

elfu

1000

Deuteronomy 1:12

Taarifa ya jumla

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli

Lakini ni kwa namna gani mimi peke yangu nibebe shehena zenu, mizigo yenu, na mizozo yenu?

Musa anatumia swali kusisitiza kwamba hawezi kutatua shida zao yeye mwenyewe. Swali hili la kejeli linaweza kutofasiriwa kama taarifa.

beba shehena zenu, mizigo yenu

Musa anazungumza kama shida za watu na malalamiko aliyohitaji kushughulikia vilikuwa vitu vizito ambavyo alikuwa amebeba.

migogoro yenu

"mabishano yenu" au "kutokubaliana kwenu"

watu wa tabia nzuri kutoka kila kabila

"watu ambayo watu wa kila kabila la Israeli huwatii"

Deuteronomy 1:15

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza kwa watu wa Israeli.

na watu wa tabia nzuri

"na watu ambao watu wako waliwaheshimu."

maelfu...mamia...hamsini...makumi

"ya makundi ya 1,000... ya makundi ya 100...ya makundi ya hamsini... na makundi ya 10"

nahodha...,maafisa

Hivi ni vyeo kwa viongozi tofauti katika serikali ya Israeli.

kabila kwa kabila

"kutoka kila kabila lenu"

hukumu kwa haki kati ya mtu na ndugu yake

"fanya sawa na maamuzi ya haki kuhusu migogoro wanaisraeli walio nayo wao kwa wao"

Deuteronomy 1:17

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na waamuzi, basi amri ni wingi.

Hautaonesha upendeleo

"Usioneshe upendeleo"

utasikia madogo na makubwa sawasawa

Huku kulikokithiri kuwili "madogo" na "makubwa" uwakilisha watu wote.

Hautaogopa uso wa mtu

Hapa neno "uso" ni neno badala ya mtu kamili. "Hauta" ni amri. "Usimuogope yeyote"

kwa wakati ule

Hii umaanisha wakati walipokuwa huko Horebu, katika mlima wa Sinai.

Deuteronomy 1:19

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israel nini kizazi cha awali cha Israel walifanya.

jangwa la ajabu mliloliona

"jangwa kubwa na hatari ambalo mlivuka"

Deuteronomy 1:20

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israel ambacho kizazi cha awali cha wanaisrael walifanya.

Tazama...Mungu wenu...mbele yenu;nenda juu, miliki...baba zenu...kwenu; usiogope, wala kukatishwa tamaa.

Musa anazungumza na wanaisraeli kama alikuwa anazungumza na mtu mmoja, basi fomu hizi zinapaswa kuwa umoja, siyo wingi.

ametayarisha nchi mbele yenu

"sasa anawapa nchi hii kwenu."

Deuteronomy 1:22

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israel nini kizazi cha awali cha wanaisraeli walifanya.

watu kumi na mbili

"12 wanaume"

Waligeuka na kwenda

"Waliondoka eneo hilo na kwenda"

bonde la Eshcoli

Hili ni bonde katika mji wa Hebroni, ambao uko kusini mwa Yerusalemu.

waliutafuta

"walitazama kwa ajili ya maeneo wataweza kuvamia"

Deuteronomy 1:25

Taarifa ya ujumla:

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israel kile kizazi cha awali cha wanaisraeli walifanya

Walichukua

"Wanaume 12 walichukua"

walichukua baadhi ya mazao ya nchi katika mikono yao

"walichukua baadhi ya mazao ya nchi"

walileta kwetu neno na kusema

Msemaji anazungumza kama vile "neno" vilikuwa vitu halisi ambavyo mtu fulani angeweza kuleta.

walisema, Ni nchi nzuri ambayo Yahwe Mungu wetu anatupa sisi!

Nukuu ya moja kwa moja inaweza kutofasiriwa kama nukuu ambayo siyo ya moja kwa moja. "kusema kuwa nchi ambayo Yahwe Mungu wetu alikuwa anatupa ilikuwa nzuri"

Deuteronomy 1:26

Taarifa ya ujumla:

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israel kile kizazi cha awali cha wanaisraeli walifanya.

Bado mlikataa kuvamia

Mungu aliwaamuru wanaisraeli kuvamia na kuwamaliza Wamorites, lakini wanaisraeli waliwaogopa na kukataa kupigana nao.

katika mkono wa Wamorites

Hapa "katika mkono" anamaanisha kuwapa Wamorites nguvu juu yao.

Tuende wapi sasa?

Hapa swali hili linasisitiza namna gani walikuwa wameogopa. Swali hili la fumbo linaweza kutofasiriwa kama maelezo.

kufanya mioyo yetu kusinyaa

Hii inamaanisha kwamba waliogopa.

na yenye boma kuelekea mbinguni

Huku ni kutia chumvi ambako kunasisitiza namna ya watu waliovyotishwa walivyokuwa kwa sababu miji ilikuwa mipana na imara.

yenye boma kuelekea juu

"kuwa na kuta ambazo ziko juu kama"

wana wa Anakimu

Hawa ni wazao wa Anak watu ambayo walikuwa wakubwa na katili

Deuteronomy 1:29

Taarifa ya ujumla

Musa aliendelea kuwakumbusha watu wa Israel nini kizazi kilichopita cha Israel kilivyofanya.

Nilikuambia

"Niliwambia mababu zenu"

mbele ya macho yenu

Hapa maneno haya "mbele ya macho yenu" urejea kile walichokiona.

ulichokiona...Yahwe Mungu wenu aliwabeba...mlienda...mlikuja

Musa anazungumza na wana Israel kama walikuwa mtu mmoja, basi mifano ya "wewe" na "vyako" ni umoja.

Yahwe Mungu wenu aliwabeba, kama mtu anavyombeba mtoto wake.

Hapa kujali kwa Yahwe kwa watu wake kunalinganishwa kama kwa baba. "Yahwe Mungu wenu amewajali, kama baba anavyomjali mtoto wake"

mpaka ulipokuja katika eneo hili

"mpaka ulipokuja katika nchi hii ambayo Mungu ameahidi kukupa"

Deuteronomy 1:32

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israel nini kizazi cha awali cha Israel kilivyofanya.

Yahwe Mungu wenu...yupi alienda mbele yenu

Musa anawakumbusha wao kwa njia za Yahwe alivyoenda mbele ya Israel wakati ya safair zao wakati zamani.

tengeneza kambi

"weka mahema yenu"

Deuteronomy 1:34

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israel nini Yahwe alivyosema nao.

alisikia sauti ya maneno yao

"alisikia kile mlikuwa mnasema"

aliapa na kusema

Mungu alifanya kiapo si kuwaruhusu wale walioasi dhidi yake kuingia nchi aliyowaahidia kuwapa.

utaona

"utaingia"

muokoe Kalebu

"isopokuwa Kalebu"

Jephunnehi

Hili ni jina la baba yake na Kalebu.

alimfuata kikamilifu Yahwe

Yahwe anazungumza kama alikuwa mtu mwingine.

Deuteronomy 1:37

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israel kile kizazi cha awali cha Israeli kilichofanya.

Yahwe alikuwa na hasira nami kwa sababu yako

Hii urejea kwa wakati Musa aliposhindwa kutii kile Yahwe alichokuwa amemwambia kufanya kwa sababu Musa alikuwa na hasira na watu wa Israel.

Nun

Hili ni jina la baba yake Yoshua

yupi asimamae mbele yako

Kwanini Yoshua anasimama mbele ya Musa kunaweza kutajwa kwa ufasaha. "yupi anasimama mbele yako kama mtumishi" au "yupi anayekusaidia"

Deuteronomy 1:39

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israel kile kizazi cha awali cha Israel kilichofanya.

hakuna maarifa mazuri au mabaya

Hawajui bado kipi kizuri na kipi kibaya.

geuka na anza safari yako

"geuka nyuma na uende tena kwa njia uliopitia"

Deuteronomy 1:41

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israel nini kizazi cha awali cha Israeli kilichofanya

kufanya dhambi dhidi ya Yahwe

"tumeasi dhidi ya Yahwe kwa kutomtii yeye"

tutamfuata

"tutamtii"

kuvamia nchi ya mlima

Hapa maneno "nchi ya mlima" uwakilisha watu ambao wanaishi huko. "kuwavamia watu wanaoshi kwenye nchi ya mlima."

kwa kuwa sitakuwa na wewe, na utashindwa na adui zako

Hii inaweza kutajwa katika kauli tendaji. "maadui zako watakushinda kwa sababu sitakuwa pamoja nawe."

Deuteronomy 1:43

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

kuvamia nchi ya mlima

Haya maneno "nchi ya mlima" husimama kwa ajili ya watu ambao wanaishi huko. "wavamie watu ambayo wanaoishi kwenye nchi ya mlima"

kuwafukuza kama nyuki

Nyuki ni mdudu mdogo, arukae kwa kundi kubwa na kuuma watu wanaowatishia. Hii inamaanisha kwamba Wamorites wengi waliwavamia askari wa Israeli kwamba wanapaswa kuacha vita.

kukupiga chini huko Seir, mbali kama Hormah

"kukupiga wewe chini katika nchi ya Seir na kukufukuza wewe mbali kama mji wa Hormah"

kukupiga wewe chini

"kuua askari wengi wako"

Deuteronomy 1:45

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israel nini kizazi cha awali cha Israeli kilichofanya.

kurudi

"kurudi Kadeshi"

Deuteronomy 2

Deuteronomy 2:1

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israel nini kizazi cha awali cha Israeli kilichofanya.

Kisha tuligeuka na kuanza safari yetu

"Kisha tuligeuka nyuma na kwenda"

tulienda nyuma Mlima wa Seir kwa siku nyingi

Maana zinazowekana ni 1) Wanaisraeli walisafiri karibu na mlima wa unaoitwa Seir kwa muda mrefu 2) Wanaisraeli walitangatanga katika mkoa unaoitwa Mlima wa Seir kwa muda mrefu.

Mlima Seir

Hili ni eneo la mlima kusuni mwa bahari mvu. Hii eneo linaitwa Edom.

siku nyingi

Lugha baadhi zinatofasiri hii kama "usiku mwingi"

Deuteronomy 2:4

Taarifa ya ujumla

Yahwe aendelea kuzungumza na Musa

wa ndugu zako, wazao wa Esau

"wa ndugu zako, wazao wa Esau"

Nimeutoa mlima Seir kwa Esau kama miliki

Yahwe anawakumbusha wanaisraeli kwamba amewapa eneo hili kwa wazao wa Esau.

Deuteronomy 2:6

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuelekeza Israel kwa namna watakavyowatendea wazao wa Esau

Utanunua chakula toka kwao

Yahwe anawapa ruhusa au maelekezo, siyo amri, na anawambia wasiibe. "Ninakuamuru kununua chakula kutoka kwao" au "kama unahitaji chakula, utanunua kutoka kwao"

kutoka kwao

"kutoka uzao wa Esau"

kwa pesa

Kama haya maneno hayaitajiki au kufanya tofasiri kutokuwa sahihi, unaweza kuyatoa.

Mungu wenu amewabariki ninyi...mikono yenu...kutembea kwenu...Mungu wenu...pamoja nanyi, na hamjapungukiwa.

Musa azungumza kwa wanaisraeli kama walikuwa mtu mmoja, basi mifano "wewe" na "vyao" ni umoja

nyie katika kazi zenu za mkono

Hii "kazi za mkono yenu" urejea kwa kazi yote waliofanya.

amejua kutembea kwenu

Hili ni neno lenye maana sawa kwa "anajua kile kilichotokea kwenu wakati mlipokuwa mnatembea."

miaka arobaini

40 miaka

hamjapungukiwa kitu chochote

Hii inatumika kama takwimu ya hotuba "umekuwa na kila kitu ulichohitaji."

Deuteronomy 2:8

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza kwa watu wa Israel.

kwa ndugu zetu

"kwa ndugu zetu"

Elathi...Ezioni Geberi

Haya ni majina ya miji

tuligeuka

"tuliendelea kwenda"

Deuteronomy 2:9

Taarifa ya ujumla

Huu ni mwisho wa sehemu wa hotuba ya Musa akiwakumbusha wanaisraeli kwa namna Yahwe alivyowaongoza jangwani.

Usiwasumbue Moabu

Neno "Moabu" ni neno lenye maana sawa na watu wa Moabu.

Ar

Hili ni jina la mji huko Moabu

uzao wa Lutu

Watu wa Israel walihusiana na uzao wa Maobu. Maobu alikuwa mtoto wa Lutu. Lutu alikuwa mpwa wa Abrahamu

Deuteronomy 2:10

Taarifa ya ujumla

Mwandishi anaanza kutoa taarifa za nyumba kuhusu watu wa nchi. Haya maneno siyo sehemu hotuba ya Musa kwa wanaisraeli.

Emim aliishi...kuwaita wao Emim

Haya maneno yanatoa taarifa ya nyuma kuhusu watu wa Emim, walioishi kwenye nchi kabla ya Moabites. Lugha yako inaweza kuwa na njia maalumu ya kuweka alama ya taarifa ya nyuma.

Emim...Rephaimu

Haya ni majina ya watu wa makundi ambayo yalijulikana kama watu wakubwa

Anakimu

Hawa ni wazao wa Anak watu waliokuwa wakubwa na katili.

Deuteronomy 2:12

Taarifa ya ujumla

Hii inaendeleza taarifa ya nyuma kuhusu watu wa makundi tofauti walioishi katika nchi.

Horites

Hili ni jina la kundi la watu

kuwateketeza wao kutoka mbele zao

"Kuwaua wote hivyo hakuna yeyote kati yao waliobaki kuishi nao" au "kuwaondoa kutoka katika uwepo wao kwa kuwaua wote"

Deuteronomy 2:13

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha wanaisraeli nini kilitokea kwao jangwani.

'Sasa inuka...Zeredi! hivyo

"Kisha Yahwe alisema, "Sasa inuka...Zeredi! hivyo" Hii inaweza kutofasiriwa kama nukuu ambayo siyo ya moja kwa moja. Kisha Yahwe alituambia kuinuka...Zeredi. Hivyo"

inuka

anza kufanya jambo fulani

kijito cha Zeredi

Mkondo huu utiririka kuelekea bahari iliyokufa kutoka kusini mashariki na utengeneza mpaka kati ya Edomu na Moabu.

Sasa siku

Neno "sasa" uweka alama ya badiliko kutoka hadithi kwenda taarifa ya nyuma kuhusu namna ya umbali wa watu wa Israel walivyotembea na kuhusu hasira ya Mungu kwa kizazi hicho. Kama lugha yenu ina njia ya kuonesha kwamba kile kifuatacho ni taarifa ya nyuma, unapaswa kuitumia hapa.

miaka thelasini na nane

miaka minane""- miaka 38

walikwisha enda kutoka kwa watu

Hii ni njia ya kusema kwa upole "amekwisha kufa."

mkono wa Yahwe ulikuwa kinyume

Hapa "mkono wa Yahwe" urejea kwa nguvu ya Yahwe. "Yahwe alitumia nguvu zake kinyume" au Yahwe aliadhibu

Deuteronomy 2:16

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israel kwa kile kilichotokea nyuma

Wewe...umekuja...usihangaike...nakupa

Musa anazungumza kwa wanaisrael kama walikuwa mtu mmoja, hivyo mifano yote "wewe" na amri "usihangaike" ni umoja

pita juu ya Ar

Hili ni jina la mji wa Moabu.

uzao wa Lutu

Hawa watu wa Israel walihusiana na uzao wa Ammoni. Ammoni alikuwa mtoto wa Lutu. Lutu alikuwa mpwa wa Abrahamu.

Deuteronomy 2:20

Taarifa ya ujumla

Hii mistari inaanza kutoa taarifa ya nyuma kuhusu makundi ya watu yaliyokwisha ishi kwenye nchi hiyo. Kama lugha yenu ina njia ya kuonesha kwamba kile kifuatacho ni taarifa ya nyuma, inapaswa itumiwe hapa.

Hilo pia linafikiriwa

Hii inaweza kutajwa katika kauli tendaji.

Rephaimu

Hili ni jina la kikundi cha watu.

Zamzummim

Hili ni jina jingine la kikundi cha watu wa Rephaim.

Anakimu

Hili ni jina la kikundi cha watu

uwaharibu wao mbele ya Ammonites

"waliruhusu Ammonites kuwashinda wao" au "waliruhusu Ammonite kuwaua wote"

waliwaondoa na kuishi katika nchi yao

"Ammonites walichukua kila kitu Rephaim walivyokuwa wamemiliki na kuishi walikoishi Rephaim"

Horites

Hili ni jina la kikundi cha watu

waliwaondoa na kuishi katika eneo lao

"kuchukua kila kitu cha watu wa Horites walivyomiliki na kuishi ambako waliishi Horites"

Deuteronomy 2:23

Taarifa ya ujumla

Mwandishi anamalizia kufafanua namna Mungu alivyomuwezesha Esau kuchukua nchi ambayo Esau anaishi kwa sasa

Avvites...Caphtorim

Haya ni majina ya makundi ya watu

Caphtor

Hili ni jina la eneo. Inaweza kuwa jina jingine la kisiwa cha Krete kinachopatikana katika bahari ya Mediterranean.

kuwaangamiza

"kuwaangamiza Avvim"

waliishi kwenye eneo lao

"waliishi ambako Avvim waliwahi kuishi"

Deuteronomy 2:24

Taarifa ya ujumla

Mwandishi amemaliza kutoa taarifa za nyuma na sasa tena anaeleza kile Musa alisema kwa wanaisraeli

Sasa inuka

Yahwe anamwambia Musa nini watu wanapaswa kufanya. "Sasa inuka" au "Sasa nenda"

nenda katika njia yako

"endelea safari yako"

bonde la Arnon

Hili ni jina la bonde la mto wa Arnon. Utengeneza mpaka kati ya Moabu na Amorites.

Nimejiweka katika mkono wako

Haya maneno "katika mkono wako" unamaanisha "kwenye utawala au nguvu yako" "Nimekupa nguvu ya kushinda"

mkono wako...Kuanza kumiliki...kupigana...kukutisha...habari kuhusu wewe...kwa sababu yako

Musa anazungumza kwa wanaisraeli kama alikuwa mtu mmoja, hivyo mifano mingi ya "wewe" na "yako" na amri " kuanza kumiliki" na "kupigana" ni umoja.

Sihoni

Hili ni jina la mfalme.

Heshboni

Hili ni jina la mji.

pigana naye

"pigana dhidi yake na jeshi lake"

weka uoga na utisho

Haya maneno "uoga" na "utisho" unamaanisha kwa msingi kitu kile kile na kusisitiza kwamba uoga ni mkubwa

watu ambao wako chini ya anga lote

Hii ni nahau "watu katika kila nchi"

kutetemeka na kuwa katika uchungu

Haya ni maelezo ya wazo moja katika maneno mawili na kusisitiza kwamba watu wata "ogopa kwa uchungu"

Deuteronomy 2:26

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israel.

Nakutuma

Hapa "na" urejea kwa Musa

jangwa la Kedemoth

Hili ni jina la eneo karibu na bonde la Arnon.

Sihon...Heshbon

Haya ni majina ya mwanaume na eneo.

pamoja na maneno ya amani

Hapa "maneno ya amani" umaanisha "pamoja na toleo la amani" au "pamoja na ujumbe kutoka kwangu kuuliza kwa ajili ya amani."

Nitageuka wala kwa mkono wa kulia wala wa kushoto.

Haya maneno yanasisitiza kwamba wakati wote wataenda kwa upande uleule. Inaweza kutajwa katika kauli chanja. "Nitageuza uelekeo" au "Nita wakati wote katika njia"

Deuteronomy 2:28

Taarifa ya ujumla

Hii inaendeleza ujumbe wa Musa kwa mfalme Sihoni

Utaniuzia chakula mimi kwa pesa, ili kwamba niweze kula; nipe maji kwa pesa, ili kwamba niweze kunywa.

Musa anamwambia Sihon kwamba wanaisraeli hawataiba kutoka kwa Amorite na maombi kwamba Sihon na watu wake wanauza chakula na maji kwa wanaisraeli; hawapi amri. "Nategemea kulipa kwa ajili ya chakula ili kwamba niweze kula na kulipa kwa ajili ya maji ili niweze kunywa"

niuzie mimi...niweze kula...nime mimi...niweze kunywa

Musa anarejea kwa watu wa Israel kama walikuwa Musa mwenyewe. "Niuzie maji na watu wangu...tuweze kula...tupe...tuweze kunywa"

pekee niruhusu nipite kwa miguu yangu

"pekee niruhusu kutembea kupitia mkono wako"

Ar

Hili ni jina la eneo.

Deuteronomy 2:30

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu kwa kile kilichotokea nyuma.

Sihoni...Heshbon

Haya ni majina ya mwanaume na eneo

Mungu wako...uwezo wako

Musa anazungumza kwa wanaisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo mifano yote ya "wewe" viko katika umoja

kufanya akili yake kuwa ngumu na kufanya moyo wake wa ukaidi

Ote maneno yanamaanisha kitu kilekile na kusisitiza kwamba Yahwe "alisababisha afanyike kaida sana."

kuwaokoa Sihon na nchi yake mbele yako

"kukupa Sihoni na nchi yake kwako"

anza kuimiliki, ili kwamba uweze kuirithi nchi yake

"chukua miliki ya nchi yake, ili kwamba uweze kuimiliki"

Deuteronomy 2:32

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israel kuhusu kile kilichotokea hapo nyuma

Sihoni

Hili ni jina la mwanaume.

Jahazi

Hili ni jina la mji wa Moabu

Deuteronomy 2:34

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu kuhusu kile kilichotokea hapo nyuma.

Tulichukua miji yake yote

"Tuliiteka miji yote ya mfalme Sihoni.

kuharibu kabisa kila mji

"kuua watu wote walioishi kwenye kila mji"

Deuteronomy 2:36

Aroer

Hili ni jina la mji ulioko kaskazini ukingoni mwa mto Arnon.

bonde la Arnon

"Arnon: ni jina la mto.

hapakuwa na mji mrefu kwetu

Taarifa hii iliyo chanya inatumika kusisitiza mafanikio yao kwenye vita. Hii inaweza kutajwa katika hali ya chanya. "tuliweza kuwashinda watu wa kila mji hata kama mji ulikuwa na kuta ndefu kuizunguka."

haukuenda

Musa anazungumza kwa wanaisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo "wewe" ni umoja

Mto Jabboki

Hili ni jina la mto ambao ulitengeneza mpaka kati ya nchi ya Sihoni na nchi ya Ammonites.

Deuteronomy 3

Deuteronomy 3:1

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israeli kwa kile kilichotokea hapo nyuma.

Ogi...Sihoni

Haya ni majina ya wafalme

Edrei...Heshbon

Haya ni majina ya miji.

Yahwe alisema nami, 'Usimuogope; ...nimekupa...chini ya utawala wako...Utafanya...kama ulivyofanya...huko Heshbon.'

Yahwe anazungumza na Musa kama Musa alikuwa mwanaisraeli, hivyo amri "usiogope" na mifano yote ya "wewe" na "yako" viko katika wingi.

muogope yeye...juu yake...watu wake na nchi yake

Hapa maneno "yeye" na "yake" urejea kwa Ogi

Nimekwisha kukupa ushindi

Yahwe anazungumza kwa kile atakachofanya kama vile amekwisha fanya.

Utafanya kwake kama ulivyofanya kwa Sihoni

Neno "kwake" ni neno la badala la "watu wake." "Utamharibu Ogi na watu wake kama ulivyofanya kwa Sihoni"

Deuteronomy 3:3

na watu wake wote waliwekwa chini ya utawala wetu

Hii inaweza kutajwa katika hali tendaji. "na Yahwe aliwaweka watu wa Ogi chini ya utawala wetu"

tulimpiga kufa

Neno "tu" urejea kwa neno badala la watu wake wote. "tuliwauwa watu wake wote"

hakuna hata mmoja wa watu wake walibaki

Hii ni neno rahisi linalotumika kusisitiza kwamba wanasraeli hawakuacha yeyote kuishi. "watu wake wote waliuwawa"

hapakuwa na mji mmoja ambao hatukuuchukua

Hii ni maradufu ya hasi ambayo inasisitiza kwamba walichukua miji 60 yote. "tulichukua kila mmoja ya miji"

miji sitini

"60 miji"

mkoa wa Argobi

Hili ni jina la mkoa ndani ya Bashani

Deuteronomy 3:5

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israel kwa kile kilichotokea hapo nyuma.

Hii ilikuwa ni miji yenye ngome yote

"Hii ilikuwa miji iliyolindwa yote"

badala ya

"kwa nyongeza" au "si pamoja"

Sihoni

Hili ni jina la mfalme.

Heshbon

Hili ni jina la mji.

kuharibu kikamilifu kila mji

"kuua watu wote walioishi kwenye kila mji"

Deuteronomy 3:8

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

nje ya mkono wa wafalme wawili

Hapa maneno "nje ya mkono wa" unamaanisha 'kutoka utawala wa." "kutoka utawala wa wafalme wawili" au "toka kwa wafalme wawili"

Amorites...Bashani...Edrei...Ogi

"Watu wa Amorite...nchi ya Bashani...mji wa Edrei...mfalme wa Ogi:

ng'ambo ya pili ya Yordani

Hii urejea kwa nchi kuvuka mto Yordani kuelekea mashariki mwa Israeli. Musa alikuwa mashariki mwa Yordani wakati aliposema hivi: "mashariki mwa mto Yordani"

Mlima wa Hermoni...Sirioni...Seniri

Haya ni majina ya mlima ule ule ambao uko kaskazini mwa mpaka wa Bashani.

ya tambarare

Hii ni juu, nchi tambarare kati ya mto Arnon na Mlima Gileadi.

Salekah

Hili ni jina la mji uliokaribu na Edrei.

Deuteronomy 3:11

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli

Kwa masalio...namna watu wanavyopima

Hii ni taarifa ya nyumba kuhusu mfalme Ogi

Tazama!

"Zingatia mambo muhimu ambayo naenda kukuambia"

Haikuwa kwa Rabbah..kuishi?

Mwandishi anatumia swali kuwakumbusha watu wa Israel kwamba wataweza kwenda Rabbab na kuona namna alivyofikia ukubwa Ogi. Hili swali linaweza kutofasiriwa kama maelezo . Maana zinazowezekana ni 1) "Ilikuwa ni huko Rabbah, ...kuishi." 2)"Ni huko Rabbah... kuishi."

thiraa

Thiraa ni sentimeta 46

namna watu wanapima

"kulingana na thiraa watu wengi wanatumia"

Deuteronomy 3:12

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu kile kilichotokea hapo nyuma.

Ni eneo lilelile linaitwa nchi ya Rephaim

Mwandishi anaanza kuwasilisha taarifa ya nyuma kuhusu nchi ambayo watu wa Israeli waliiteka. Kama lugha yenu ina namna ya kuonesha kwamba kile kinachofuata ni taarifa ya nyuma, unapaswa kuitumia hapa.

Deuteronomy 3:14

Taarifa ya ujumla

Hii inaendeleza taarifa ya nyuma kuhusu nchi ambayo watu wa Israeli waliiteka.

Jair

Hili ni jina la mwanaume.

Geshunites na Maacathites

Haya ni makundi ya watu walioishi magharibi mwa Bashani.

Havvoth Jair

Mtofasiri anaweza kuweka maelezo haya kwa kusema: "Jina la 'Havvoth Jair' linamaanisha 'mahema ya kijijini Jair' au 'ulimwengu wa Jair"

Deuteronomy 3:15

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Nilimpa

Hapa "Ni" urejea kwa Musa.

kwa Machir

"kwa uzao wa Machir." Huyu ni mwana wa Manasseh. Alikufa kabla Musa hajatoa nchi hii.

bonde la Arnon

Hili ni jina la bonde la mto wa Arnon. Inatengeneza mpaka kati ya Moabu na Amorites.

Mto Jabbok

Hili ni jina la mto ambao ulitengeneza mpaka kati ya nchi ya Sihoni na nchi ya Ammonites.

Deuteronomy 3:17

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli

Moja ya mipaka mingine pia

"Mpaka wa magharibi wa Rubeni na wilaya ya Gadi"

Chinnerethi

"bahari ya mchumvi." Hili ni eneo sawa kama "Bahari ya Galilaya" au "Ziwa la Genesareti"

Mlima Pisgah

Hili ni jina la mlima huko sehemu ya kaskazini wa mlima Abarimu

Deuteronomy 3:18

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Nilikuamuru kwa wakati huo

Musa anawakumbusha kabila la Reubeni, kabila la Gadi, na nusu ya kabila la Manasseh kwamba wanapaswa kuwasaidia waisraeli wengine kushinda nchi ambayo Mungu aliwaahidi.

tutapita tukiwa na silaha mbele

"tutachukua silaha zao na kuvuka mto Yordani mbele yao"

ndugu zenu, watu wa Israeli

"ndugu zenu wanaisraeli"

Deuteronomy 3:19

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza kwa makabila ya Reuben na Gadi na nusu ya kabila la Manasseh.

Yahwe awapa ndugu zenu pumziko

Mwandishi anazungumza kama uwezo wa kupumzika ulikuwa ni suala la kimwili ambalo linaweza kutolewa kama zawadi. Neno "pumziko" pia ni mfano kwa maisha ya amani ambayo hayana vita. "Yahwe awaruhusu ndugu zenu kupumzika" au "Yahwe awaruhusu ndugu zenu kuacha kupigana vita na kuishi kwa amani"

ng'ambo ya Yordani

Hii inarejea kwa nchi kuvuka mto Yordani, mashariki mwa Israeli. Musa alikuwa mashariki mwa Yordani wakati aliposema hiki. "mashariki mwa mto Yordani."

kisha utarudi

Musa anasisitiza kwamba makabila mengine yanapaswa kumiliki maeneo yao kabla ya Yahwe ataruhusu haya makabila matatu kumili nchi yao. "kisha mtarudi peke yenu."

Deuteronomy 3:21

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israeli kuhusu kile kilichotokea huko nyuma.

Macho yako yameona

Hapa "macho" urejea kwa Yoshua.

Deuteronomy 3:23

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu kuhusu kile kilichotokea huko nyuma

Niliwasihi

Hapa "Ni" urejea kwa Musa. Hii inamaanisha alimuuliza Mungu kwa uhodari kabisa, kihisia.

kumuonesha mtumwa wako

Hapa "mtumwa wako" ni njia ya utulivu kuzungumza kwa mwingine na mamlaka makubwa.

mkono wako wa nguvu

Hapa neno "mkono" umaanisha utawala au nguvu.

kwa mungu yupi hapo...matendo?

Musa anatumia swali kusisitiza kwamba Yahwe ni Mungu pekee aliye na nguvu kufanya kazi alizozifanya. Swali hili linaweza kutofasiriwa kama maelezo. "kwa kuwa hakuna mungu...matendo."

huko mbinguni au duniani

Huku kulikothiri mara mbili kwa pamoja unamaanisha "popote."

Ng'ambo ya Yordani

"magharibi mwa mto Yordani." Wakati Musa alizungumza haya maneno kwa Yahwe, alikuwa mashariki mwa mto Yordani huko Moabu.

Deuteronomy 3:26

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwaambia watu wa Israel kile kilichotokea huko nyuma

Yahwe alikasirika juu yangu kwa sababu

Hii inarejea kwa wakati Musa hakutii kile Yahwe alimwambia kufanya kwa sababu Musa alikuwa amewakasirikia watu wa Israeli.

inua macho yako

Haya maneno "Inua macho yako" yako ni maneno ambayo yana maanisha kutazama.

Deuteronomy 3:28

Taarifa ya ujumla

Yahwe aendelea kuzungumza na Musa

Betho Peor

Hili ni jina la mji huko Moab karibu na mlima Pisgah

Deuteronomy 4

Deuteronomy 4:1

Ni karibu kukufundisha

Musa anawambia watu wa Israeli kile Mungu anataka wao kufanya.

kuwafanyia

"na kuwatii"

Hautayaongeza maneno ...wala kuyapunguza

Yahwe hataki watu wake kutengeneza sheria mpya, au kupuzia zile alizowapa tayari.

Deuteronomy 4:3

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli

Macho yako yameona

Hapa "macho" urejea kwa watu wa Israeli

Kwa sababu ya Baali Peor

Maana kamili ya maelezo haya yanaweza kufanywa wazi. "kwa sababu ya dhambi ulifanya kwa Baali Peor"

Yahwe Mungu wako amewaangamiza kutoka kwenu

Musa anazungumza kwa watu wa Israeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo "yako" na "wewe" ni umoja.

wewe ulimshikilia Yahwe

Mwandishi anazungumza kama kumtegemea Yahwe na kumtii yeye kulikuwa kama kumshikilia mtu kimwili.

Deuteronomy 4:5

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Tazama

"Zingatia"

kwamba ufanye hivyo katikati mwa nchi

"kwamba uwatii wakati unaishi kwenye nchi"

zishike na kuzifanya

Haya makundi mawili ya maneno kwa msingi yana maanisha vilevile na kusisitiza kwamba watawaitii.

hii ni hekima yako na uelewa wako kwa mtazamo wa watu

Maneno "hekima" na "uelewa" ni maneno mbadala wa imani ya watu kwamba wanaisraeli walikuwa na hekima na uelewa kwa kile cha umuhimu. "hiki ndicho kitaonesha watu hekima yako na uelewa wako"

machoni pa watu

Maneno "machoni pa" unamaanisha "kwa mtazamo wa." Hii inamaanisha watu wengine watawatazama watu wa Israel kuwa na hekima.

hili taifa kubwa ni la watu wa hekima na uelewa.

Neno "taifa" ni neno kwa kwa ajili ya watu wa taifa hilo.

Deuteronomy 4:7

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli

Kuna taifa gani jingine la vile liko hapo ...yeye? Kuna taifa gani jingine kubwa la vile liko hapo...leo?

Haya maswali yanaweza kutofasiriwa kama maelezo. "Kwa kuwa hakuna taifa kubwa jingine...yeye. Hakuna taifa kubwa jingine leo."

Deuteronomy 4:9

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Zingatia peke na kuwa makini ... kujilinda, usisahau ... macho yako... moyo wako ... maisha yako... yafanye yajulikane kwa watoto wako na wana watoto wako ... uliyosimama mbele ya Yahwe Mungu wako

Musa anazungumza kwa wanaisraeli kama alikuwa mtu mmoja, hivyo mifano ya "wewe", "yako" na "mwenyewe," "linda," na "fanya ujulikane" ni umoja.

Zingatia kwa pekee na kwa makini ujilinda,

"Zingatia kwa makini na uwe na uhakika kukumbuka haya mambo daima"

usisahau...haziuwachi moyo wako

Haya maneno umaanisha kitu kilekile na kusisitiza kwamba watu wa Israel wanapaswa kukumbuka kile walichokiona.

macho yako yameoana

Hapa "macho " inasimama kwa nafsi.

Nikusanyie watu

"Walete watu kwa pamoja na walete kwangu"

Deuteronomy 4:11

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha wanaisraeli historia yao.

pamoja na moto kwa moyo wa mbinguni

Haya maneno "Moyo wa" unamaanisha " katikati ya" au "sehemu ya ndani zaidi," na "mbingu" hapa urejea kwa anga. "pamoja na moto ambao ulienda angani"

kwa giza, mawingu, na giza nene

Hapa "giza nene" uelezea mawingu. "kwa nene, wingu la giza"

giza nene

Maana nyingine ni "wingu zito"

Deuteronomy 4:13

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza kwa watu wa Israeli.

Alitangaza

"Yahwe alitangaza"

kwako

Hapa "kwako" urejea kwa wanaisraeli walioenda kwenye mlima Horebu.

katika nchi ambayo ulikuwa unavuka kuchukua miliki ya

"baada ya kuvuka mto wa Yordani na kuchukua miliki ya nchi"

Deuteronomy 4:15

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu Israeli

Kwa hiyo chukua tahadhari kubwa mwenyewe

Maana 1) "Kwa hiyo unahitaji kuwa makini namna unavyotenda" au 2) "Linda nafsi yako kwa makini."

usiwe fisadi mwenyewe

"usifanye kile kilichokibaya"

huenda kwa ardhi

tambaa juu ya ardhi"

Deuteronomy 4:19

Hautainua macho yako...na kutazama... na kusogezwa... Yahwe Mungu wako

Musa anazungumza kwa wanaisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo mifano yote ya "wewe" na "yako" na maneno "inua," "tazama," na "kusogezwa" ni umoja.

Hautainua ... na kusogezwa mbali kuabudu

Hii inaweza kutofasiri katika kauli. "Usi... na usimwaache yoyote akufanye uabudu" au " Usi...na usikubali mwenyewe kuabudu"

jeshi lote la mbinguni

"chochote unachoweza kuona angani." Hii ni njia nyingine wa kurejesha kwa jua, mwezi, na nyota.

ambayo Yahwe Mungu wenu amewapa ushiriki watu wote

Hii ni nahau. Musa anazungumza juu ya nyota kama zilikuwa vitu vidogo kama chakula ambacho Yahwe alikuwa anagawa na kuwapa makundi ya watu. "kwamba Yahwe Mungu wenu ameweka hapo kusaidia makundi yote ya watu."

aliwatoa kutoka tanuru la chuma

Musa anazungumza juu ya Misri na kazi ngumu wanaisraeli walifanya huko kama vile oveni ambayo chuma kinachomwa na wanaisraeli walikuwa ni chuma.

Deuteronomy 4:21

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza kwa watu wa Israeli.

Yahwe alikuwa amekasirika juu yangu kwa sababu

Hii inarejea wakati Musa alishindwa kutii kile Yahwe alimwambia kufanya kwa sababu Musa alikuwa amekasirika juu ya watu wa Israeli. Maana kamili ya maelezo haya inaweza kufanywa wazi.

Yahwe Mungu wenu anawapa

Musa anazungumza kwa wanaisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo "wewe" na "wako" ni umoja.

Deuteronomy 4:23

Zingatia mwenyewe

"Zingatia kwa makini"

Yahwe Mungu wenu amewakataza... Yahwe Mungu wenu

Musa anazungumza kwa wanaisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno, "wewe" na "wako" ni umoja.

Yahwe Mungu wenu ni Mungu wa moto wa mawindo, wivu.

Musa analinganisha namna Yahwe anafanya wakati anakasirika kwa njia ya moto unavyoharibu vitu. " Yahwe Mungu wenu atawahukumu kwa ukali na kuwaharibu kama moto ufanyavyo kwa sababu hataki muwabudu miungu mingine"

Deuteronomy 4:25

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

unazaa... Yahwe Mungu wenu

Maneno "wewe" na "wako" ni umoja hapa.

kuzaa

unakuwa baba wa, au unakuwa babu wa

kama mnakuwa na tabia mbaya wenyewe

"kama mnafanya vibaya." maneno ya kufanana yanaonekana katika 4:15

na fanya kile kilicho kibaya mbele ya Yahwe Mungu wenu, kumkasirisha hasira yake

Hii ni nahau. "na unamfanya Yahwe Mungu wenu kukasirika kwa kufanya kile anachosema ni kiovu"

Naita mbingu na dunia kushuhudia

Maana zinazowezekana ni 1) Musa anaita wote wale wanaoishi mbinguni na duniani kuwa mashahidi kwa kile anachosema au 2) Musa anazungumza na mbingu na dunia kama walikuwa watu, na anawaita kuwa mashahidi kwa kile anachokisema.

utaziongeza siku zako

Siku ndefu ni mfano wa maisha marefu.

lakini utaangamiza kabisa

Kama inavyoonyeshwa katika 4:27, si kila mwisraeli atauwawa. Hapa "kuharibu kabisa" ni kusisitiza kwamba wanaisraeli wengi watakufa. "lakini Yahwe atawaangamiza wengi wao"

Deuteronomy 4:27

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Yahwe atawatawanyisha miongoni mwa watu

Musa anazungumza kama watu walikuwa mbegu ambayo Yahwe ataitawanyisha kuzunguka eneo. "Yahwe atawatuma ninyi kwa maeneo mengi tofauti na kuwalazimisha kuishi huko"

atawaongoza mbali

"atawatuma" au "atasababisha adui zenu kuwapeleka mbali"

kazi ya mikono ya watu, mbao na mawe

Hapa "mikono ya watu" urejea kwa wanaume wenyewe, na "kazi...mbao na mawe" kwa sanamu ambazo wamezichonga. "sanamu za mbao na mawe ambazo wanaume wamefanya"

Deuteronomy 4:29

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli. Anazungumza kama walikuwa mtu mmoja, hivyo mifano yote ya "wewe" na "wako" ni umoja.

Lakini kutoka huko

"Lakini wakati mlipokuwa katika mataifa yale mengine"

utatafuta

Neno "u" hapa ni wingi.

wakati utakapo nitafuta

"wakati unapojaribu kumtafuta yeye" au " wakati unajaribu kumjua yeye"

kwa moyo wako na nafsi yako

Hii ni nahau "kwa ote....moyo" unamaanisha "kabisa" na pamoja na ote...nafsi" umaanisha "na utu wetu wote." Haya maneno yana maana ile ile.

Deuteronomy 4:30

yatakuwa yamekuja

"yametokea kwa"

katika siku zile

"baada ya hapo" au "kisha"

sikiliza sauti yake

Hapa "sikiliza" ina maana kusikia na kutii, na "sauti yake" urejea kwa Yahwe na kile anachosema. "tii kile anachosema"

Deuteronomy 4:32

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo mifano yote ya "wewe" na amri "uliza sasa" ni umoja.

Imeshawahi watu kusikia ya Mungu anazungumza katikati mwa moto, kama umekwisha sikia, na kuishi?

Hapa watu wa Israeli wanakumbushwa kwa namna Yahwe amezungumza nao kwa njia ya ajabu siku za nyuma. Hili swali linaweza kutofasiriwa kama maelezo.

sikiliza sauti ya Mungu anazungumza

Neno "sauti" ni maneno kwa ajili ya Mungu, alikuwa anazungumza. "Sikiliza sauti ya Mungu azungumzapo"

Deuteronomy 4:34

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli

na kwa mkono wa ushujaa, na kwa mkono ulionyoshwa

Hapa "mkono wa ushujaa" na "mkono kunyoshwa" ni mifano ya nguvu ya Yahwe.

mbele ya macho yenu

Hapa "macho" urejea kwa mtu mzima

Deuteronomy 4:35

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo mifano yote ya "wewe" na "wako" ni umoja.

Kwako mambo haya yalionyeshwa

Hii inaweza kutajwa katika kauli tendaji. "Yahwe aliwaonyesha mambo haya"

aliwafanya kusikia...aliwafanya kuona

"alihakikisha mnasikia...alihakikisha mmeona"

kuwafanya ... mlisikia

Musa anazungumza kama watu waliokuwa anaongea nao walikuwa ni watu alioongea nao kwenye mlima Sinai miaka mingi ya mwanzoni. Watu katika mlima Sinai kwa uhalisia walikuwa baba wa watu ambayo alikuwa anaongea maneno haya.

Deuteronomy 4:37

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu Israeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo mifano yote ya "wewe" na "yako" ni umoja.

baba zako

Hii inarejea kwa Abraham, Isaka, Yakobo, na wana wa Yakobo.

pamoja na uwepo wake, pamoja na nguvu zake kuu

"pamoja na nguvu kuu ambayo huja kutoka kwenye uwepo wake" au "pamoja na nguvu kuu"

Deuteronomy 4:39

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo mifano yote ya "wewe" na "yako" ni umoja

iweke juu ya moyo wako

Hii ni nahau. "ikumbuke"

mbinguni zaidi na chini ya dunia

Haya maneno "mbinguni" na "duniani" uonyesha kukubwa kuwili na ina maanisha "kila sehemu."

kuongoza siku zako

Siku ndefu ni mfano wa maisha marefu. "kuweza kuishi maisha marefu."

Deuteronomy 4:41

Taarifa ya ujumla

Hotuba ya Musa, ambayo inaanza katika 1:5, imekwisha,na mwandishi aendelea na simulizi ambayo inakoma katika 1:5

Bezeri... Ramothi... Golani

Haya ni majina ya miji

Deuteronomy 4:44

Hii ni sheria

Hii inarejea kwa sheria za Musa zitakazotelewa katika sura zifuatazo.

Beth Peori

Hili ni jina la mji huko Moabu karibu na mlima Pisgah.

Sihoni...Amorites... Heshboni

"Mfalme Sihoni...watu wa Amorite...mji wa Heshboni."

Deuteronomy 4:47

nchi yake

nchi ya mfalme Sihoni

ng'ambo ya Yordani kuelekea mashariki...upande wa mashariki ng'ambo ya Yordani

Hii inarejea kwa nchi kuvuka mto Yordani, kuelekea mashariki mwa Israeli. Musa alikuwa Mashariki mwa Yordani wakati aliposema hivi. "kutoka upande wa mto Yordani kuelekea mashariki... upande wa mashariki kutoka upande wa mto Yordani"

Aroeri

Hili ni jina la mji.

bonde la Arnon

Hili ni jina la eneo.

Mlima Sioni...Mlima Hermoni

Haya ni majina ya milima.

Deuteronomy 5

Deuteronomy 5:1

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

kuitwa kwa Israeli yote

Musa alitaka kila mmoja Israeli kusikiliza na kutii maneno yake, lakini sauti yake inawezekana haikuwa kubwa kwamba kila mmoja kumsikia.

kwamba nitazungumza katika masikio yenu leo

Hapa "masikio" urejea kwa mtu ote. Huu mfano unasisitiza kwamba watu wanajua kile Musa alichosema kwao, ili kwamba wasitende dhambi na kisha wasiseme hawakujua kuwa walikuwa wanafanya dhambi.

Yahwe hakufanya agano hili na baba zenu

Maana zinawezekana ni 1) Yahwe hakufanya pekee agano na wale waliokuwa huko Horebu; agano pia lilikuwa na kizazi cha badae cha Israeli au 2) Yahwe hakufanya agano hili na baba zenu wa mbali, kama vile Abrahamu, Isaka, na Yakobo; badala yake, agano hili lilianza na wanaisraeli huko Horebu.

Deuteronomy 5:4

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

ana kwa ana

Tumia lugha ya mifano kwa watu wawili ambao wana karibiana na kutazamana wakati wanazungumza wao kwao wao.

juu ya mlima

"juu ya mlima"

kwa wakati huo

Musa anarejea kwa tukio ambalo lilitokea yapata miaka 40 ya mapema.

nje ya nyumba ya utumwa

Hapa maneno "nyumba ya utumwa" urejea kwa Misri ambako watu wa Israeli walikuwa watumwa.

Deuteronomy 5:7

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu kile Yahwe amewaamuru. Maneno "uta" na "hauta" amriwa. Anazungumza na wanaisraeli kama vile walikuwa mtu mmoja.

Hamtakuwa na miungu mingine mbele zangu

"Haupaswi kuabudu miungu yoyote lakini mimi"

hiyo iko chini ya dunia, au hiyo iko chini ya maji

Hii inaweza kufanywa kwa uwazi. "kwamba iko katika dunia chini ya miguu, au iko kwenye mahi chini ya dunia"

Deuteronomy 5:9

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo mifano yote ya "wewe" na "yako" ni umoja.

Hautavipigia magoti au kuvitumia

"Hautaabudu sanamu za kuchonga au fanya kama wanavyowa waamrisha"

Hauta

"Hapana"

Mimi...ni Mungu wa wivu

"Mimi...nataka mniabudu mimi pekee"

kwa maelfu, kwa wale wanapendao

Tofasiri zingine usoma " kwa vizazi elfu ambao wananipenda." Neno "elfu" ni mfano wa namba inayozidi kuhesabu.

Deuteronomy 5:11

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo mifano ya "wewe" na "yako" ni umoja

Hautalichukua jina la Yahwe

"Hautalitumia jina la Yahwe"

kwa utupu

"kutojali" au "kutokuwa na heshima sahihi" au "kwa kusudi baya"

Yahwe hatamshikilia kuwa ana hatia

Hii inaweza kutajwa katika hali chanya. "Yahwe atamchukulia kuwa ana hatia" au "Yahwe atamhukumu"

Deuteronomy 5:12

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo mifano yote ya "wewe" na "yako" ni umoja

kuiweka takatifu

"weka wakfu kwa Mungu"

fanya kazi yako yote

"fanya majukumu yako za kawaida"

siku ya saba

"Siku ya 7" Hapa "siku ya saba" ni namba ya kawaida kwa ajili ya saba

Juu yake hautafanya

"Siku ile usifanye"

ndani ya malango yako

Hapa "malango" ni rejeo ya mji wenyewe. "ndani ya jamii yako" au " ndani mji wako" au "kuishi pamoja nanyi"

Deuteronomy 5:15

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo mifano yote ya "wewe" na "yako" ni umoja

Utaita akilini

Huu ni mfano. "Unapaswa kukumbuka"

kuwa mkono hodari na mkono ulionyoshwa

Hapa "mkono hodari" na "mkono uluonyoshwa" ni mifano ya nguvu za Yahwe. Tofasiri hii kama ilivyo katika 4:34.

Deuteronomy 5:16

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo mifano yote ya "wewe" na "yako" ni umoja

Deuteronomy 5:17

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo mifano yote ya "wewe" na "yako" ni umoja

Hautazini

"Hautalala na yoyote tofauti na mwenzi wako"

Hautashuhudia uongo dhidi ya jirani yako

"Hautasema uongo kuhusu mtu yeyote"

Deuteronomy 5:21

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo mifano yote ya "wewe" na "yako" ni umoja

Deuteronomy 5:22

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israeli kile alichosema Yahwe.

Deuteronomy 5:23

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israeli kile kilichotokea nyuma

kusikia sauti

Neno "sauti" ni maneno kwa ajili ya mlio wa sauti au kwa ajili ya mtu aliyekuwa anazungumza. "kusikia mlio wa sauti" au "kusikia Yahwe anazungumza"

Deuteronomy 5:25

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha wanaisraeli kile walichokuwa wamesema kwa Musa

Lakini tufe?

Walikuwa wameogopa kwamba watakufa kama alizungumza nao. Hili swali linaweza kutofasiriwa kama maelezo. "Tunaogopa kuwa tutakufa"

Nani badala yetu yuko hapo...amefanya?

Hili swali linaweza kutofasiriwa kama maelezo. "Hakuna watu badala yetu...wamefanya"

nyama yote

Hili ni neno kwa ajili ya "watu wote" au "viumbe vyote."

Deuteronomy 5:28

wakati ulipozungumza na mimi

Hapa "mimi" urejea kwa Musa

Oh, kwamba walikuwa

Kama lugha yako ina maneno ya kueleza hamu ya nguvu kwa ajili ya kitu fulani, unaweza kutumia hapa.

Deuteronomy 5:31

Taarifa ya ujumla

Yahwe aendelea kuzungumza na Musa

utawafundisha

"utawafundisha watu wa Israeli"

Deuteronomy 5:32

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Utaishika

Musa anawapa amri watu wa Israeli.

hautageukia mkono wa kulia wala kushota

Hii inalinganisha mtu kutomtii Mungu na mtu kuiacha njia sahihi.

kuongeza siku zako

Siku ndefu ni mfano wa maisha marefu.

Deuteronomy 6

Deuteronomy 6:1

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea na hotuba kwa watu wa Israeli anaanza 5:1. Kuanzia mstari wa 2, anazungumza na watu wa Israeli kama walikuwa mtu mmoja.

kushika kwa nguvu...kushika

"utii kwa nguvu...kutii"

kwenda zaidi ya Yordani

"kwenda upande mwingine wa mto Yordani"

kwamba siku zako ziweze kuongezeka

Siku ndefu ni mfano wa maisha marefu. Hii inaweza kutajwa kwa kauli tendaji. Hii inaweza kutofasiriwa sawasawa na "kuongeza siku zako" 4:25 "kwamba niweze kuongeza siku zako" au "kwamba nikusababishe uishi muda mrefu"

Deuteronomy 6:3

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwambia watu wa Israeli maneno ya Yahwe kama wanaisraeli walikuwa mtu mmoja.

wasikilize wao

Hapa "wasikilize" ina maana kutii, na "wao" urejea kwa amri za Yahwe. Maana kamili ya maelezo haya yanaweza kufanya wazi. "sikiliza amri za Yahwe, sheria na amri"

kuwatii wao

"watii wao"

nchi itiririkayo maziwa na asali

Hii ni nahau. "nchi ambako maziwa na asali ya wingi utiririka" au " nchi ambayo iko vizuri kwa mifugo na kilimo"

Deuteronomy 6:4

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwambia watu wa Israeli maneno ya Yahwe kama wanaisraeli wako mtu mmoja.

Yahwe Mungu wetu ni mmoja

"Mungu Yahwe wetu ni mmoja na pekee Mungu"

kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, na nguvu zako zote

Haya maneno yaliounganishwa yanasisitiza kwamba mtu anapaswa kumpenda Mungu kabisa na kwa ukamilifu kujitoa kwake.

Deuteronomy 6:6

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwambia watu wa Israeli maneno ya Yahwe kama wanaisraeli walikuwa mtu mmoja.

Ninakuamuru wewe

Musa anazungumza amri za Mungu kwa watu wa Israeli

itakuwa katika moyo wako

Hii ni nahau. "unapaswa daima kukumbuka"

utafundisha kwa bidii... utaongea

"Ninakuamuru wewe kufundisha kwa bidii...Ninakuamuru wewe kuongea." Msomaji anapaswa kuelewa haya kama amri.

Deuteronomy 6:8

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwaambia watu wa Israeli maneno ya Yahwe kama wanaisraeli wako mtu mmoja.

yafunge

Hii ni neno kwa ajili ya "andika haya maneno kwenye ngozi, weka ngozi kwenye mkoba, na ufunge mkoba." Hili ni neno kwa nyogeza linaweza kuwa mfano kwa ajili ya "kutii haya maneno ili iwe kama yalikuwa kimwili hapo."

kama ishara juu ya mkono wako

"kama kitu fulani kufanya wewe kukumbuka sheria zangu"

nazo zitatumika kama utepe

Hii ni neno kwa ajili ya "andika haya maneno kwenye ngozi, weka ngozi kwenye mkoba, na ufunge mkoba kwenye kichwa chako ili ukae." Hili ni neno kinyume linaweza kuwa mfano kwa ajili ya "kutii haya maneno ili kwamba iwe kama vile vilikuwa katika uhalisia hapo."

utepe

mapambo mtu uvaa kwenye paji la uso

Utaandika

Hii ni amri

Deuteronomy 6:10

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwaambia watu wa Israeli maneno ya Yahwe kama wanaisraeli wako mtu mmoja.

kubwa na miji mizuri sana ambayo hamkujenga

Miji hii yote itakuwa ya watu wa Israeli wakati wanawateka watu wa Canaan.

nje ya nyumba ya utumwa

Hapa maneno "nyumba ya utumwa" urejea kwa Misri, eneo ambalo watu wa Israeli walikuwa watumwa.

Deuteronomy 6:13

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwaambia watu wa Israeli maneno ya Yahwe kama wanaisraeli wako mtu mmoja.

Utamheshimu Yahwe Mungu wako; yeye utamwabudu, na utaapa kwa jina lake

"Ni Yahwe Mungu wenu na hakuna mmoja mwingine ambaye mtaheshimu; ni yeye peke yake ambaye mtamwabudu, na ni kwa jina lake na jina lake pekee mtaapa." Lugha yenu inaweza kuwa na njia nyingine ya kusisitiza kwamba Yahwe anawaambia wanaisraeli kutomwabudu au kumtumikia mungu mwingine.

utaapa kwa jina lake

Kuapa kwa jina la Yahwe ina maana kumfanya Yahwe msingi au nguvu ambayo inatumiwa kufanya kiapo. Maneno "jina lake" urejea kwa Yahwe mwenyewe.

katikati yenu

"ambaye anaishi miongoni mwenu"

hasira ya Yahwe Mungu wenu itawashwa dhidi yenu

Musa analinganisha hasira ya Yahwe na yeyote anawasha moto kuharibu vitu. Hii inaweza kutajwa kwa kauli tendaji. Kuwasha hasira ni mfano wa kuwa na hasira sana.

kuwaharibu ninyi toka

"kuwaharibu ili kwamba hakuna chochote kilichobaki kwenu popote"

Deuteronomy 6:16

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwaambia watu wa Israeli maneno ya Yahwe kama wanaisraeli wako mtu mmoja.

Hauta mjaribu Yahwe

Hapa "kujaribu" ina maana kutoa changamoto kwa Yahwe na kumlazimisha kujithibitisha.

Massah

Hili ni jina la eneo huko jangwani. Mtofasiri anaweza kuongeza maneno kusema: "Jina la 'Massah' umaanisha 'kujaribu'

Deuteronomy 6:18

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwaambia watu wa Israeli maneno ya Yahwe kama wanaisraeli wako mtu mmoja.

Utafanya kilicho sawa na kizuri mbele ya Yahwe

Hii nahau ni amri na baraka. Kama wanaisraeli wanamtii Yahwe, watapokea baraka kutoka kwa Yahwe.

Deuteronomy 6:20

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwaambia watu wa Israeli maneno ya Yahwe kama wanaisraeli wako mtu mmoja

Ni zipi amri za agano...amrisha ninyi

Hili swali ni maneno. "Nini amri za agano...aliamuru umaanisha kwako" au "Kwanini tunapaswa kutii amri za agano...amrisha ninyi"

mwana wako

Hii urejea kwa watoto wa watu wakubwa wa Israeli ambao Musa alikuwa anazungumza maneno ya Yahwe.

na mkono hodari

Hapa "mkono hodari" urejea kwa nguvu ya Yahwe/

na juu ya nyumba yake yote

Hapa maneno "nyuma yake" urejea kwa watu wa Yahwe.

mbele za macho yenu

Hapa neno "macho" urejea kwa mtu kamili

kuweza kutuleta sisi ndani

Maana kamili ya maelezo haya inaweza kufanywa wazi.

Deuteronomy 6:24

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwaambia watu wa Israeli maneno ya Yahwe kama wanaisraeli wako mtu mmoja. Anawaambia kile wanachopaswa kuwaambia watoto wao kuhusu amri za Yahwe.

mbele ya Yahwe

"katika uwepo wa Yahwe" au "wapi Yahwe anaweza kutuon sisi"

shika

"tii"

hii itakuwa haki yetu

Hili ni neno. "atatuangalia sisi wenye haki"

Deuteronomy 7

Deuteronomy 7:1

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwaambia watu wa Israeli maneno ya Yahwe kama wanaisraeli wako mtu mmoja.

Deuteronomy 7:2

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwaambia watu wa Israeli maneno ya Yahwe kama wanaisraeli wako mtu mmoja.

anawapa ninyi ushindi juu yenu

Musa anazungumza ushindi kama vile ulikuwa kitu halisi mtu mmoja angeweza kumpa mwingine.

juu yao

Hapa "wao" urejea kwa mataifa saba kutoka

Deuteronomy 7:4

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwaambia watu wa Israeli maneno ya Yahwe kama wanaisraeli wako mtu mmoja.

Kwa watakuwa

"Kama mtaruhusu watoto wenu kuoa watu kutoka mataifa mengine, watu kutoka mataifa watakuwa"

Kwa hiyo hasira ya Yahwe itawashwa dhidi yenu

Musa analinganisha hasira ya Yahwe kwa yeyote anawasha moto. Hii inasisitiza nguvu ya Yahwe kuharibu kile kimsababisha yeye kukasirika. Hii inaweza kutajwa katika kauli tendaji.

dhidi yenu

Neno "wewe" urejea kwa wanaisraeli wote na kwa hiyo ni wingi.

utashughulika...utavunja...kata..choma

Musa anazungumza na wanaisraeli wote, kwa hiyo haya maneno ni wingi.

Deuteronomy 7:6

Taarifa ya ujumla

Musa awaambia watu wa Israeli maneno ya Yahwe kama wanaisraeli wako mtu mmoja.

u taifa lililowekwa wakfu

Yahwe kuchagua watu wa Israeli kuwa watu wake katika njia maalumu inazungumzwa kama Yahwe kuwatenga toka mataifa mengine.

ambao wako juu wa uso wa dunia

Hii ni nahau. "ambao uishi juu ya dunia"

Deuteronomy 7:7

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwaambia watu wa Israeli maneno ya Yahwe. Mifano yote ya "wewe" na "yako" ni uwingi.

hakuweka upendo wake juu yenu

"hakuwapenda ninyi"

pamoja na mkono hodari

Hapa "mkono hodari" urejea kwa nguvu ya Yahwe.

kuwakomboa toka nyumba ya utumwa

Musa anazungumza juu ya Yahwe kuwakomboa watu wa Israeli kutoka katika utumwa kama vile Yahwe amelipa pesa kwa mmiliki wa mtumwa.

nyumba ya utumwa

Hapa maneno "nyumba ya utumwa" urejea kwa Misri, eneo ambalo watu wa Israeli walikuwa watumwa.

mkono wa Farao

Hapa "mkono" una maana "utawala wa" "utawala wa Farao"

Deuteronomy 7:9

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwaambia watu wa Israeli maneno ya Yahwe kama wanaisraeli wako mtu mmoja.

kwa vizazi elfu

"kwa 1,000 kizazi"

walipe wale wanaomchukia kwenye uso wao

Hii nahau ina maanisha "kuwalipa kwa haraka na uwazi ili kwamba wajue Mungu amewaadhibu."

hatakuwa na huruma kwa yeyote anayemchukia

"Yahwe atawahukumu kwa ukali wowote wanaomchukia"

Deuteronomy 7:12

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwaambia watu wa Israeli maneno ya Yahwe. Anazungumza kama vile wanaisraeli wako mtu mmoja katika mstari wa 12 na kwa wote wale kama kundi katika mstari 13.

na kuwazidisha

"na kuongeza idadi ya watu wako"

matunda ya mwili wako

Hii ni nahau kwa ajili ya "watoto wako"

matunda ya ardhi yako

Hii ni nahau kwa "mazao yako"

kuzidisha kwa mifugo yako

"mifugo yako hivyo itakuwa mingi"

Deuteronomy 7:14

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwaambia watu wa Israeli maneno ya Yahwe kama vile wanaisraeli wako mtu mmoja.

Utabarikiwa zaidi kuliko watu wengine wote

Hii inaweza kutajwa katika kauli tendaji. "Nitakubariki zaidi kuliko ninavyowabariki watu wengine wowote."

hapatakuwa na utasa wa kiume au wa kike miongoni mwenu au miongoni mwa mifugo yenu

Musa atumia maelezo hasi kusisitiza kwamba wote wataweza kuwa na watoto. Hii inaweza kutajwa katika hali chanya. "Wote ninyi mtaweza kuwa na watoto na mifugo wataweza kuzaa"

miongoni mwenu...mifugo

Maneno haya "wewe" na "yako" viko katika wingi.

chukua mbali na magonjwa yako yote

"hakikisha haumwi" au "jiweke kabisa na afya"

hakuna hata magonjwa mabaya ... atakayoweka juu yenu, lakini atayaweka juu ya wale wanaomchukia.

Musa anazungumza kama ugonjwa ulikuwa kitu kizito ambacho Yahwe angeweka juu ya watu. "

Deuteronomy 7:16

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwaambia watu wa Israeli maneno ya Yahwe kama wanaisraeli wako mtu mmoja.

Mtaondoa makundi ya watu wote

"Ninakuamuru kuharibu kabisa makundi ya watu wote"

jicho lako halitawaonea huruma

Hii ni amri. Musa azungumza kama vile jicho lionavyo lilikuwa jicho lenyewe. "Usiruhusu kile unachoona kusababisha kuwahurumia" au "usiwe na huruma kwa sababu ya kile unachofanya kinawaumiza"

hautaabudu

"kamwe kuabudu"

kwamba itakuwa mtego kwako

Kama watu wanaabudu miungu mingine, watakuwa kama mnyama aliyeshikwa kwenye mtengo wa mawindo, na hawataweza kutoroka.

Deuteronomy 7:17

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwaambia watu wa Israeli maneno ya Yahwe kama wanaisraeli wako mtu mmoja.

Kama unasema kwenye moyo wako... usiogope

Watu hawapaswi kuogopa hata kama wanagundua kwamba mataifa yako na nguvu kuliko wao. "Hata kama mnasema moyoni mwenu"

sema kwenye moyo wako

"fikiri"

namna gani ataweza kuwafukuza wao?

Musa atumia swali kusisitiza kwamba watu wataweza kujihisi kuogopa mataifa mengine. Hili swali linaweza kutofasiriwa kama maelezo. "Siwezi kuwashinda wao"

mtafikiri akilini

Hii ni nahau. "unapaswa kukumbuka"

kile macho yenu yameona

Hapa "macho" urejea kwa watu walichoona.

mkono hodaru, na mkono ulionyoka

Hapa "mkono hodari" na "mkono ulionyoka" ni mifano ya nguvu ya Yahwe

Deuteronomy 7:20

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwaambia watu wa Israeli maneno ya Yahwe kama wanaisraeli wako mtu mmoja.

Zaidi ya hayo

"Na pia"

tuma nyigu

Yamkini maana ni 1)Mungu atatuma wadudu walikuo ambao wanauuma watu na kusababisha maumivu, au 2) Mungu atasababisha watu kuogopa na kutaka kukimbia.

kuangamia kutoka uweponi mwako

"kufa ili usiwaone tena"

Hautakuwa

"Kamwe"

mkuu na Mungu wa kutisha

"mkuu na Mungu wa kutisha" au "Mungu mkuu asababishae watu kuogopa"

kidogo kwa kidogo

"polepole"

Deuteronomy 7:23

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwaambia watu wa Israeli maneno ya Yahwe kama wanaisraeli wako mtu mmoja.

kuwapa ninyi ushindi

"kuwawezesha ninyi kushinda"

ushindi juu yao

Ushindi juu ya majeshi toka mataifa mengine"

atawachanganya kabisa

"atawafanya wao ili wasiweze kufikiri vizuri"

mpaka waangamizwe

Hii inaweza kutajwa katika kauli tendaji.

utafanya jina lao kuangamia toka chini ya mbingu

Wanaisraeli kabisa watawaangamiza watu toka mataifa hayo, na mbeleni hakuna atakayewakumbuka.

kusimama mbele yenu

"kusimama dhidi yako" au "kujitetea wao dhidi yenu"

Deuteronomy 7:25

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwaambia watu wa Israeli maneno ya Yahwe. Katika mstari wa 25 azungumza na makundi kama makundi, kwa hiyo mifumo ya "wewe" viko kwa wingi, lakini mstari wa 26 azungumza kama wanaisraeli wako mtu mmoja, kwa hiyo mifumo iko kwa umoja.

Utachoma

Hii ni amri

miungu yao

"miungu ya mataifa mengine"

usitamani...utanaswa nayo

Haya maneno yaongeze kwa maelekezo ya kuchoma sanamu.

utanaswa nayo

Hata kama kuchukua dhahabu na fedha kwenye sinamu kungesababisha watu kuanza kuiabudu. Kwa kufanya hivyo watakuwa kama mnyama aliyeshikwa kwenye mtego. Hii inaweza kutajwa katika mfumo tendaji.

kwa kuwa ni chukizo kwa Yahwe Mungu wenu

Haya maneno uwambia kwanini Yahwe ataka watu kuchoma sanamu. "fanya hivi kwa sababu Yahwe Mungu achukua sana"

Kwa hakika utachukizwa na kuzuia

Maneno "kuchukiza" na "chukia" kwa msingi umaanisha kitu kile kilie na kusisitiza kiwango cha chukizo.

kwa kuwa imetengwa kwa ajili ya uharibifu

Yahwe analaani kitu fulani na kuahidi kukiharibu kama ilinavyozungumzwa kama Yahwe alikuwa anaweka kitu fulani tofauti na kila kitu. Hii inaweza kutajwa kwa mfumo tendaji. :"kwa kuwa Yahew amekwisha tenga kwa maangamizi"

Deuteronomy 8

Deuteronomy 8:1

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na wanaisraeli kama walikuwa mtu mmoja

Unapaswa kushika...uweze kuishi na kuongozeka, na kuingia ndani na kumiliki...baba zenu

Mifano yote ya "wewe" na "yako" na vitendo viko kwa wingi

miaka arobaini

"miaka 40"

apate kuwanyenyekeza

"apate kuwaonyesha ninyi namna mlivyo dhaifu na wenye dhambi"

Utafakari akilini

Hii ni nahau. "Unapaswa kukumbuka"

kujua

"kudhihirisha" au "kuonyesha"

nini kilikuwa katika moyo wenu

Moyo ni ishara ya tabia ya mtu.

Deuteronomy 8:3

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na wanaisraeli kama walikuwa mtu mmoja. Aendelea kuwakumbusha nini wanapaswa "kutafakari akilini"

Aliwanyenyekeza

"Yahwe aliwaonyesha namna mlivyo dhaifu na wenye dhambi" Ona namna "anaweza kuwanyenyekeza" imetofasiriwa katika 8:1

aliwalisha kwa manna

"aliwapa manna kula"

si kwa mkata tu kwamba watu waishi

Hapa "mkate" uwakilisha chakula. "chakula si kitu pekee watu wanahitaji ili waishi"

ni kwa kila kitu ambacho hutoka kinywani mwa Yahwe ambacho watu wanaishi

Hapa "kinywani mwa Yahwe" ni maneno ya Yahwe anayosema. "watu wanapaswa kutii amri za Yahwe ili kwamba waweze kuishi" au " watu wanapaswa kufanya kila Yahwe awaambia kufanya ili kwamba waweze kuishi"

Deuteronomy 8:4

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na wanaisraeli kama walikuwa mtu mmoja.

Mavazi yenu...miaka arobaini

Hiki ni kifungu cha mwisho wanapaswa kukumbuka "tafakari akilini"

miaka arobaini

"miaka 40"

Utafikiri...Utashika... tembea katika njia zake na kumheshimu

Hii yaendeleza orodha ya amri ambazo zimeanza katika 8:1

Utafikiri kuhusu katika moyo wako

Hapa neno "moyo" uwakilisha mawazo na uelewa wa mtu.

Deuteronomy 8:7

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na wanaisraeli kama walikuwa mtu mmoja

nchi ya

"nchi pamoja" au "nchi ambayo ina"

Deuteronomy 8:9

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na wanaisraeli kama walikuwa mtu mmoja.

nchi ambayo mtakula mkate pasipo kupungukiwa

"nchi ambapo kutakuwa chakula kingi kwa ajili yenu"

ambapo hautaenda pasipo kuwa na kitu

Hii inaweza kutajwa katika mfumo chanya. "ambapo utakuwa na kila kitu unachohitaji"

mawe yaliyotengenezwa kwa chuma

Mawe yaliyojaa madini ya chuma. Chuma ni kigumu utumika kwa upanga na plau.

chimba shaba

"mgodi wa shaba." Shaba chuma kiliani utumika kwa kutengenezea vyombo vya nyumbani.

Mtakula na kushiba

"Mtakuwa na chakula cha kutosha kula mpaka mnashiba"

mtabariki

"mtasifu" au "mtatoa shukrani kwa"

Deuteronomy 8:11

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumzza na wanaisraeli kama walikuwa mtu mmoja.

usipuuzie amri zake

"usiache kutii amri zake" au "kuendelea kutii amri zake"

Uwe makini kwamba, wakati unakula... ishi kwazo

Musa aanza kuwaambia kitu cha pili wanachohitaji kuwa makini nacho. Hii ni orodha ndefu ambayo inaendelea katika mistari ifuatayo.

Uwe makini kwamba, wakati unakula na kushiba, na wakati unajenga

Yamkini maana nyingine ni kwamba hizi si "wakati" vishazi lakini ni mbadala ya mwanzo wa orodha ya matokeo ya kuupuzia amri za Yahwe: "Kama unapuuzia amri zake, utakula na kushiba na kujenga."

wakati unapokula na unashiba

"wakati unakuwa na chakula cha kutosha kula"

Deuteronomy 8:13

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na wanaisraeli kama walikuwa mtu mmoja.

wakati kundi la wanyama...dhahabu inaongezeka

Haya maneno ni ya mwisho katika orodha ya "wakati" vishazi ambavyo huanza pamoja na "wakati unakula" 8:11

kundi la wanyama wako na mifugo yako

"kundi la ng'ombe wako na kundi la kondoo wako na mbuzi"

kuongezeka

"kuongezeka kwa namba" au "kuwa wengi"

vyote ambavyo umezidisha

"una vitu vingi zaidi" au "una umiliki mwingi zaidi"

kwamba wakati ule moyo wako ulipoiunuliwa... ulimsahau Yahwe

Musa ambia mambo mawili ambayo yatatokea kama wote "wakati" maelezo 8:11 yanakuwa kweli.

moyo wako umefanyika kuinuliwa juu

Hii ni nahau "unaweza kuwa na kiburi"

nani alikuleta nje

Musa anaanza kuwakumbusha wanaisraeli kwa kile wanachojua kuhusu Yahwe.

nje ya nyuma ya utumwa

Huu ni mfano wa wakati walipokuwa watumwa huko Misri.

Deuteronomy 8:15

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na wanaisraeli kama walikuwa mtu mmoja.

nani aliwaongoza...huko mwishoni

Musa aendelea kuwakumbusha wanaisraeli kwa kile wanachojua kuhusu Yahwe

na kupitia

"na kuwaongoza kupitia"

nyoka wa moto

"nyoka wa sumu"

ardhi ya kiu

Haya maneno yanaelezea ardhi kuwa na kiu kama vile mtu anavyokuwa na kiu wakati anapohitaji maji. "ardhi kavu"

nani aliongoza...nani alileta...nani alimlisha

"Yahwe, ndiye aliongoza...Yahwe,ndiye aliyeleta...Yahwe, ndiye alimlisha"

kukufanya wewe vizuri

"kukusaidia wewe" au "kwasababu itakuwa vizuri kwako"

na unasema moyoni mwako

Hili ni jambo la tatu watu wanaweza kufanya wakati mioyo yao "kuinuliwa juu" na wana "msahau Yahwe" 8:13. Hapa "moyo" ni maneno mbadala wa mawazo ya ndani ya mtu.

Nguvu yangu na mkono hodari wangu umepata utajiri wote huu.

Hapa "mkono" urejea kwa nguvu za mtu au uwezo. "Nimepata utajiri huu kwa sababu niko imara na nguvu" au "Nimepata vitu hivi vyote kwa nguvu zangu na uwezo wangu"

Deuteronomy 8:18

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na wanaisraeli kama walikuwa mtu mmoja.

Lakini utafikiri akilini

Hii nahau ni amri. "Lakini kumbuka"

kwamba aweze

"kwa hiyo anaweza"

kwamba aweze kuanzisha

Yamkini maana ni 1) "kwa njia hii anaanzisha" au 2) "kwa njia hii ni mwaminifu kuanzisha."

kuanzisha

"kutimiza" au "kushika"

kama ilivyo leo

"kama anavyofanya sasa" au "kama anavyoanzisha agano lako sasa"

tembea baada ya miungu mengine

kutembea ni mfano wa kutii. "tumikia miungu mingine"

dhidi yako...uta...mbele yako...utaangamia...usinge...Mungu wako

Hii ni mifano ya "wewe" viko kwenye uwingi.

Nashuhudia dhidi yako

"Ninakuonya" au "Nakwambia mbele ya mashahidi "

utaangamia hakika

"hakika utakufa"

mbele yako

"mbele yako wewe"

hautasikiliza sauti ya Yahwe

Hapa "sauti ya Yahwe" ina maana kwamba Yahwe awambia watu wako kufanya.

Deuteronomy 9

Deuteronomy 9:1

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na wanaisraeli kama wako mtu mmoja.

Sikia, Israeli

"Sikiliza, watu wa Israeli." Neno "Israeli" ni maneno kwa ajili ya watu wa Israeli.

kuwafukuza

"kuchukua ardhi toka"

kuimarisha juu ya mbingu

Huku ni kutia chumvi ambako kunasisitiza namna watu waliogopa walivyokuwa kwa sababu miji ilikuwa mkubwa na imara. "ilikuwa na kuta ndefu"

Mwana wa Anakimu

Wazao wa Anak watu waliokuwa wakubwa na wakali.

Nani anaweza kusimama mbele ya wana wa Anak?

Hii ina maana kwamba wana wa Anak walikuwa na nguvu na watu waliwaogopa. Hili ni swali la kejeli linaweza kutofasiriwa kama maelezo. "Hakuna yeyote anayeweza kutetea mwenyewe dhidi ya wana wa Anaki."

Deuteronomy 9:3

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na wanaisraeli kama wako mtu mmoja.

leo

"sasa"

kama moto ulao

Yahwe ana nguvu na kuweza kuharibu majeshi ya mataifa mengine.

kuwaitiisha mbele zenu

"kuwafanya kuwa dhaifu ili muweze kuwatawala"

Deuteronomy 9:4

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na wanaisraeli kama wako mtu mmoja.

Usiseme katika moyo wako

Hapa "katika moyo wako" ina maana "katika mawazo yako"

amewatupa nje

"amewaondoa watu wengine nje"

Deuteronomy 9:5

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na wanaisraeli kama wako mtu mmoja.

unyofu wa moyo wako

"kwa sababu daima unafikiri na kutamani vitu sahihi"

ili kwamba aweze kufanya kuwa kweli neno

Hapa ni maneno "neno" urejea kwa kile Mungu ameahidi."ili kwamba aweze kutimiza ahadi"

babu zenu, Abrahamu, Isaka, na Yakobo

Abrahamu, Isaka, na Yakobo ni "mababu" ambao Musa anazungumza

Deuteronomy 9:6

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na wanaisraeli kama wako mtu mmoja.

Deuteronomy 9:7

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na wanaisraeli kama wako mtu mmoja.

Kumbuka na usisahau

Musa arudia amri ile ile vyote kwa chanya na hasi kusisitiza umuhimu wa kukumbuka.

namna mlivyomchochea Yahwe

Hapa "wewe" urejea kwa wanaisraeli ambao wako pamoja na Musa na pia wanaisraeli wa kizazi cha nyuma.

mlikuja eneo hili, mmekuwa waasi...mmechochea...pamoja na wewe kuharibu wewe

Mifano ya "wewe" ni uwingi.

kwenye eneo hili

Hii irejea kwenye mto Yordani wa bondeni.

Deuteronomy 9:9

Taarifa ya ujumla

Musa anawakumbusha watu wa Israeli nini kilitokea nyuma.

mbao za jiwe, mbao za agano ambalo Yahwe alifanya na ninyi

Hapa kikundi cha maneno ya pili ufafanua kwamba "mbao za jiwe" ni zile Mungu aliandika amri kumi.

siku arobaini na usiku arobaini

"siku 40 na usiku 40"

juu yake ziliandikwa kila kitu kama maneno yote ambayo Yahwe alitangaza kwenu

Hii inaweza kutofasiriwa katika kauli tendaji. "Yahwe aliandika juu yake maneno yale yale aliyosema kwenu"

Yahwe alitangaza...nje katikati ya moto

Ilikuwa kama Yahwe alikuwa mtu anasimama katikati mwa moto na kuzungumza kwa sauti kubwa.

katika siku ya kusanyiko

Nomino kufikirika "kusanyiko" inaweza kuelezwa kama tendo "kusanya kwa pamoja." "katika siku wakati ninyi wanaisraeli wote mlikuja na kukutana pamoja eneo moja"

Deuteronomy 9:11

siku arobaini na usiku arobaini

"siku 40 na usiku arobaini"

mbao mbili za jiwe, mbao za agano

Kundi la maneno la pili ufafanua kwamba "mbao mbili za jiwe" ni zile ambazo Mungu aliandikwa amri kumi .

watu wako...wamekuwa wafisadi wenyewe

"watu wako...wanafanya kile kilichokibaya."

Wamegeuka kwa haraka kando nje ya njia amgayo niliwaamuru

Musa azungumza kama kutii amri za Mungu walikuwa wanatembea kando ya njia. "Tayari wameshindwa kutii amri zangu"

Deuteronomy 9:13

kuyafuta majina yao toka chini ya mbingu

"kufanya majina yao kupotea kabisa" au "kuwauwa wote ili asiwepo mmoja atakayewakumbuka."

Deuteronomy 9:15

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israeli kile kilichotokea nyuma

tazama

Neno "tazama" hapa uonesha kwamba Musa alishangazwa kwa kile alichokiona

mmejitengenezea wenyewe ndama

Wanaisraeli wa kizazi cha mwanzo walikuwa wamemuuliza Aaaroni kutengeneza ndama wa chuma ili wamwabudu. Maana kamili ya maelezo haya yanaweza kuwekwa wazi.

Umegeuka kwa haraka kando nje ya njia ambayo Yahwe alikuwa amekuamuru.

Musa azungumza kama kutii amri za Mungu kulikuwa kutembea kando ya njia. "Kwa haraka umeshindwa kutii kile Yahwe alichokuwa amekuamuru."

Deuteronomy 9:17

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israeli kuhusu kile kilichotokea zamani.

Niliwavunjwa mbele ya macho yenu

Hapa "macho yenu" ni neno lenye maana sawa na watu wa Israeli.

kulala kifudifudi

"kulala pamoja na uso wangu kuelekea kwenye ardhi." Hii ni njia ya kuonesha kwamba Yahwe alikuwa mkuu na Musa hakuwa.

siku arobaini na usiku arobaini

"siku 40 na usiku 40"

Deuteronomy 9:19

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israeli kile kilichotokea zamani.

Kwa kuwa nilikuwa nimeogopa hasira na gadhabu kali ambayo Yahwe alikuwa amekasirika vya kutosha dhidi yenu kuwaangamiza

Maneno "hasira na gadhabu kali" ni mbadala wa kile Yahwe atafanya kwa sababu ya hasira na kuchukizwa. "Yahwe aliwakasirikia ninyi - alichukizwa sana nanyi-- alikasirika vya kutosha kuwaangamiza ninyi, na kwa hiyo niliogopa kwa kile atakifanya"

Deuteronomy 9:21

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israeli kuhusu kile kilichotokea zamani

Nilichukua...kuchoma...kupiga....arhini...kuwatupa

Yamkini Musa aliwaamuru watu wengine kufanya kazi halisi.

dhambi zenu

ndama wa dhahabu. "sanamu mlifanya dhambi kwa kumtengeneza"

Deuteronomy 9:22

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israeli kuhusu kile kilichotokea zamani

Taberah...Massah...Kibrothi...Hattaavah

Haya ni majina ya maeneo ambayo watu wa Israeli walipita wakati wakiwa jangwani.

Nenda juu

Walikuwa kwenye nchi ya chini, na nchi Yahwe alikuwa amekwisha waambia kuichukua ilikuwa kwenye mlima, kwa hiyo walipaswa kwenda juu ya mlima kuichukua.

waliasi dhidi ya amri

Neno "amri" ni mbadala wa Yahwe mwenyewe. "Mliasi dhidi ya Yahwe; hamkutii amri"

sikiliza sauti yake

Hapa "sauti yake" ina maana kile Mungu alikwisha sema.

kutoka siku ambayo nilikujua

"kutoka muda nilianza kukuongoza wewe." Tofasiri zingine usoma "kutoka siku ambayo nilikujua wewe," siku ambayo Yahwe kwanza aliwajua.

Deuteronomy 9:25

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israeli kuhusu kile kilichotokea zamani.

lala kifudifudi mbele ya Yahwe

"lala pamoja na uso kuelekea kwenye ardhi."

siku arobaini na usiku arobaini

"siku 40 na usiku 40"

umekwisha okoa

Musa azungumza kama Yahwe amekwisha kuwaokoa wanaisraeli kwa kulipa pesa kuwaweka huru kutoka utumwani.

kupitia ukuu wako

Neno "ukuuu" ni mbadala wa maneno kwa ajili ya nguvu kuu ya Yahwe.

kwa mkono hodari

Hapa "mkono hodari" urejea kwa nguvu ya Yahwe.

Deuteronomy 9:27

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuomba kwa Yahwe ili aweze kuwaharibu watu wa Israeli.

Akilini

Hii ni nahau. "Kumbuka"

ili kwamba nchi ambayo ulitutoa

Maneno "nchi" ni maneno kwa ajili ya watu wa Israeli.

wapate kusema

"waweze kusema"

kwa nguvu zako kuu na kwa kuonesha mamlaka yako,

Haya maneno kwa msingi umaanisha kitu kile kile na kusisitiza ukuu wa nguvu za Yahwe ambao aliutumia kuwaokoa watu wake.

Deuteronomy 10

Deuteronomy 10:1

Taarifa ya ujumla:

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israeli kuhusu kile kilichotokea zamani.

Kwa wakati ule

"Baada ya kumaliza kuomba"

kwanza

"kwanza: ni namba ya makutano kwa moja. Urejea kwa seti ya kwanza ya mbao ambazo Musa alizokuwa amevunja.

juu ya ule mlima

Hapa "mlima ule" urejea kwa mlima Sinai.

Deuteronomy 10:3

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israeli kuhusu kile kilichotokea zamani

kama kwanza

Hapa "kwanza" urejea kwa mbao za kwanza za jiwe. "kama mbao mbili za kwanza za jiwe"

alienda juu ya mlima

"alienda juu ya mlima Sinai"

nje katikati ya moto

Ilikuwa kama Yahwe alikuwa mtu anasimama katikati mwa moto na kuzungumza kwa sauti kubwa.

kwenye siku ya kusanyiko

Nomino ya kufikiri "kusanyiko" inaweza kuelezwa kama tendo "kusanya pamoja"

Deuteronomy 10:5

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israeli kuhusu kile kilichotokea zamani.

Niligeuka

Hapa "Ni" urejea kwa Musa.

kuja chini kutoka kwenye mlima

kuja chini kutoka kwenye mlima Sinai"

kwenye safina

"kwenye boksi" au "kwenye kifua"

Deuteronomy 10:6

Taarifa ya ujumla

Mwandishi atoa sababu fupi wapi wanaisraeli walikuwa wamesafiri.

Watu wa Israeli...nchi yenye vijito vya maji

Hii utupa taarifa ya nyuma kuhusu wapi watu wa Israeli walisafiri. Pia inagusa kifo cha asili cha Moserathi.

Beerothi Bene Jaakani kwa Moserathi...Gudgodah...Jotbathah

Haya ni majina ya maeneno tofauti watu wa Israeli walipita wakati wakiwa jangwani.

Beerothi Bene Jaakan

Mtofasiri anaweza kuongeza maelezo: "Jina 'Beerothi Bene Jaakan' umaanisha "visima ambavyo vilikuwa vya watu wa Jaakan."

huko alizikwa

Hii ina kutofasiriwa kwa kauli tendaji. "Huko ndiko walikomzika" au wanaisraeli walimzika huko"

Eleazari

Hili ni jina la mwana wa Aaroni

Deuteronomy 10:8

Taarifa ya ujumla

Mwandishi atoa taarifa ya nyumba kuhusu kabila la Lawi.

kusimama mbele ya Yahwe kumtumikia

"kutoa dhabihu ambayo Yahwe anahitaji"

katika jina lake

"kwa mamlaka ya Yahwe" au "kama mwakilishi wa Yahwe"

kama leo

"kama wanavyofanya leo"

hakuna sehumu wala urithi wa nchi

Kabila la Lawi hawakupokea sehemu ya ahadi ya nchi wakati walipofika huko. Maana kamili ya maelezo haya inaweza kuwekwa wazi.

Yahwe ni mrithi wake

Yahwe azungumza kwa mahusiano maalamu ambayo Aaron na uzao wake watakuwa pamoja naye kama Yahwe alikuwa kitu watakachoridhi.

Yahwe Mungu wenu

Musa azungumza na wanaisraeli kama wako mtu mmoja, hivyo neno "wewe" hapa ni umoja.

kuzungumzwa kwake

"kuzungumzwa kwa kablia la Lawi."

Deuteronomy 10:10

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu wa Israeli kuhusu kile kilichotokea zamani.

kama kwa wakati wa kwanza

"kwanza" ni namba ya makutano kwa ajili ya moja. Hapa urejea kwa wakati wa kwanza Musa alienda juu kwenye mlima wa Sinai kupokea mbao mbili toka Yahwe. "kama nilivyofanya kwanza"

siku arobaini na usiku arobaini

"siku 40 na usiku 40"

kuwaharibu

Musa azungumza na wanaisraeli kama wako mtu mmoja, hivyo neno "wewe" hapa ni umoja.

kumiliki nchi

"chukua nchi" au "chukua miliki ya nchi"

mababu wenu

Hii inarejea kwa Abrahamu, Isaka, na Yakobo

kuwapa wao

"ambacho nitawapa ninyi, wazao wao"

Deuteronomy 10:12

Taarifa ya ujumla

Musa anazungumza na wanaisraeli kama wako mtu mmoja.

Sasa, Israeli

Hapa neno "Israeli" urejea kwa watu wa Israeli.

nini Yahwe Mungu wenu uhitaji kwenu, isopokuwa kumuogopa...kwa uzuri wenu

Musa atumia swali kuwafundisha watu wa Israeli. Hili swali la kejeli linaweza kutofasiriwa kama maelezo. "hiki ndicho Yahwe Mungu wenu uhitaji ninyi kufanya: kumuogopa...kwa uzuri wenu

kutembea katika njia zake zote

Musa azungumza kama kumtii Yahwe kulikuwa kutembea kwenye njia.

kwa moyo wenu wote na roho yenu yote

Hii nahau "kwa moyo wenu wote" umaanisha "kabisa" na "kwa roho yenu" umaanisha "kwa utu wenu wote." Haya maneno yana maana ileile.

Deuteronomy 10:14

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na wanaisraeli kama wako mtu mmoja.

Tazama

Neno "tazama" usisitiza kwamba kile kilichosemwa badae ni muhimu. "Zingatia" au "Tazama" au "Sikiliza"

mbingu...ardhi

Haya maneno yanaonyesha kubwa mbili, na yameunganishwa kumaanisha kwamba vitu vyote popote ni mali ya Yahwe.

mbingu za mbingu

Hii urejea kwa maeneo ya juu zaidi huko mbinguni. Kila kitu mbinguni ni mali ya Mungu.

alikuchagua wewe

Hapa neno "wewe" urejea kwa wanaisraeli wote na liko kwa wingi.

Deuteronomy 10:16

Kwa hiyo

"Kwa sababu hii"

kutaili govi la moyo wako

Neno "govi" urejea kwa ngozi iliyojikunja kwa sehemu ya siri ya mwanaume ambayo uondolewa wakati wa kutaili. Hapa Musa anarejea kwa utalili wa kiroho. Hii ina maana watu wanapaswa kuiondoa dhambi toka maishani mwao.

Mungu wa miungu

"Mungu mkuu" au "Mungu pekee wa kweli"

Bwana wa bwana

"Bwana mkuu" au "Bwana mkuu"

wa kutisha

"yeye anayesababisha watu kuogopa"

Deuteronomy 10:18

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Nitafanya haki kwa yatima

"Yahwe anahakikisha kwamba watu wanafanyia haki yatima"

yatima

Hawa ni watoto ambao wazazi wote wamekwisha kufa na hawana ndugu wa kuwajali.

mjane

Mjane wa kweli ni mwanamke ambaye mme amekwisha kufa na hana watoto wa kumjali kwa umri wake wa uzee.

Kwa hiyo

"Kwa sababu hii"

Deuteronomy 10:20

Taarifa ya ujumla

Musa azungumza na wanaisraeli kama wako mtu mmoja, hivyo mifano yote "wewe" na "wako" ni umoja.

yeye mtamwabudu

"ni yeye mnayepaswa kumwabudu"

Kwake mnapaswa kushikamana

Kuwa na uhisiano mzuri pamoja na Yahwe na kumtegemea kabisa yeye aliyezungumzwa kama watu walikuwa wanashikama kwa Yahwe. "Unapaswa kumtegemea" au "Ni yeye unayepaswa kumtegemea"

kwa jina lake utaapa

Kuaapa kwa jina la Yahwe kuna maanisha kumfanya Yahwe msingi au nguvu ambayo kiapo kitafanywa.

ambacho macho yako yameona

Hapa "macho" urejea kwa mtu kamili.

Yeye ni sifa yenu

Yamkini maana ni 1) "Ni yeye unapaswa kumsifu" au 2) "Ni kwa sababu unamwabudu yeye kwamba watu wengine watamsifu yeye"

Deuteronomy 10:22

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli kama wako mtu mmoja, hivyo "wewe" na "wako" viko kwa umoja.

alienda chini Misri

"alisafiri kusini mwa Misri" au "alienda Misri"

watu sabini

"watu 70"

nyingi kama nyota za mbinguni

Hii inasisitiza namba kubwa wanaisraeli ambao walikuwa na Musa.

Deuteronomy 11

Deuteronomy 11:1

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

daima shika

"daima tii"

Deuteronomy 11:2

ambao hawajui wala hawajaona

"ambao hawajapata uzoefu"

mkono wako hodari, au mkono wake ulionyoshwa

Hapa "mkono hodari" na "mkono ulionyoshwa" ni mifano kwa ajili ya nguvu ya Yahwe. Maneno yaleyale yanaonekana katika 4:34.

katikati mwa Misri

"katika Misri"

kwa nchi yake yote

Hapa "nchi" uwakilisha watu. "kwa watu wake wote"

Deuteronomy 11:4

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza kwa wanaisraeli wakubwa ambao walikuwa na umri wa kutosha kuona yale Mungu alifanya huko Misri.

Wala hawakuona kile alichofanya

"Wala hawakuona watoto wao kile alichofanya Yahwe"

jeshi la Misri

"Wanajeshi wa kimisri"

waliwashawishi baada yao

Hapa "yao" umaanisha wanaisraeli ambao waliishi miaka 40 mapema.

kwa eneo hili

Hii inamaanisha tambarare ya bonde la mto Yordani ambako Musa anazungumza nao kabla ya kuvuka kuingia Kanani

Deuteronomy 11:6

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuwakumbusha watu wakubwa kuwafundisha watoto wao matendo makubwa ya Mungu.

Dathani na Abiramu, wana Eliabu

Musa anarejea kwa tukio la zamani wakati Dathani na Abiramu waliasi dhidi ya MUsa na Aaroni. Maana kamili ya maelezo haya inaweza kufanywa wazi.

Dathani...Abiramu...Eliabu

Haya ni majina ya wanaume

mwana wa Reubeni

"uzao wa Reubeni"

ardhi ilifungua mdomo wake na kuwameza

Yahwe anasababisha nchi kugawanyika kufungua ili kwamba watu waanguke ndani ilizungumzwa kama nchi ilikuwa na mdomo na uwezo wa kumeza watu.

kila kiumbe hai kilichowafuata

Hii urejea kwa watumishi wao na wanyama

katikati mwa Isralie yote

Hii ina maanisha watu wote wa Israeli walishuhudia kile kilichotokea kwa Dathani, Abiramu, familia zao, na miliki zao.

Lakini macho yenu yameona

Hapa "macho" uwakikilisha mtu kamili

Deuteronomy 11:8

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

kumiliki nchi

"chukua nchi"

kule unaenda katika kuimiliki

Maneno haya "unaenda katika" inatumika kwa sababu ya watu wa Israeli watapaswa kuvuka mto Yordani kuingia Kanani.

kuongeza siku zenu

Siku ndefu ni mifano ya maisha marefu.

nchi imiminikayo maziwa na asali

Hii ni nahau. "nchi ambayo maziwa na asali ya kutosha yanamiminika" au "nchi ambayo iko vizuri kwa mifugo na kilimo"

Deuteronomy 11:10

kuimwagilizia kwa mguu yao

Yamkini maana ni 1) "mguu" ni neno ambalo linawakilisha kazi ngumu ya kutembea kubeba maji kwa mashamba au 2) wangeweza kutumia miguu yao kugeuza gurudumu la maji ambalo linatoa maji kwa mashamba.

bustani ya mimea

"bustani ya mboga" au "bustani ya mboga mboga"

kunywa maji ya mvua ya mbiguni

Nchi inapokea na kufyonza vya kutosha mvua inazungumzwa kama nchi inakunywa maji.

macho ya Yahwe Mungu wenu daima yako juu yake

Hapa "macho" uwakilisha uangalifu na utunzaji

tokea mwanzo wa mwaka kwenda mwishoni mwa mwaka

Hapa kubwa hizi mbili "mwanzo" na "mwisho" zinatumiwa kwa pamoja kumaanisha mwaka mzima.

Deuteronomy 11:13

Itatokea, kama

Hii ina maana kwamba kile Yahwe anachoahidi kitatokea kama wanaisraeli wanatii amri zake.

ambayo nakuamuru

Hapa "na" urejeaa kwa Musa.

kwa moyo wako wote na roho yako yote

Hii nahau "kwa moyo wako wote" umaanisha "kabisa" na "kwa ...roho" umaanisha "na utu wako wote" Haya makundi ya maneno yana maana ileile.

Nitatoa mvua kwa nchi yenu kwa majira yake

"Nitasababisha inyeshe kwenye nchi yenu kwa majira sahihi"

Nitatoa

Hapa "ni" urejea kwa Yahwe. Hii inaweza kutajwa katika nafsi ya tatu.

mvua ya awali na mvua ya badae

Hii urejea kwa mvua za mwanzo wa majira ya kupanda na mvua za kukomaza mazao kwa ajili ya mavuno.

Deuteronomy 11:16

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli

Zingatia mwenyewe

"Uwe makini" au "jihadhari"

ili kwamba moyo wako usidanganywe

Hapa "moyo" uwakilisha hamu ya mtu au mawazo. Hii inaweza kutajwa kwa kauli tendaji.

unageuka upande na kuabudu miungu mingine

Kumkataa Yahwe na kuabudu miungu mingine inazungumzwa kama mtu anayeweza kugeuka kimwili na kwenda mwelekeo mwingine mbali na Yahwe.

ili kwamba hasira ya Yahwe iwashwe dhidi yenu

Mungu kuwa na hasira inazungumzwa kama ilikuwa ni moto ambao unaanza. Hii inaweza kutajwa kwa kauli tendaji. "ili kwamba Yahwe asiwe na hasira nanyi"

ili kwamba asifunge mbingu ili kwamba hapatakuwa na mvua, na nchi haitazaa matunda

Mungu anasababisha kukosekana mvua kudondoka toka angani inazungumzwa kama alikuwa anafunga anga.

Deuteronomy 11:18

yaweke haya maneno yangu ndani ya moyo na roho yako

Mtu daima ufikiri kuhusu na kuzingatia kile Musa aamuru inazungumzwa kama vile moyo na roho vilikuwa ni chombo cha maneno ya Musa yalikuwa ni maudhui kujaza chombo

haya maneno yangu

Hapa "maneno" uwakilisha amri za Musa ambazo anazungumza.

moyo wako na roho

Hapa "moyo: na "roho" uwakilisha akili ya mtu au mawazo.

zifunge

"yafunge haya maneno" Neno hili uwakilisha mtu akiandika maneno kwenye ngozi, kuweka ngozi kwenye mkoba, na kuufunga mkoba. Hili neno linaweza kuwa mfano kumaanisha watu wanapaswa kuwa waangalifu kutii amri za Musa.

kama ishara kwenye mkono wako

"kama kitu cha kukufanya wewe kukumbuka sheria zangu"

yawe utepe katikati ya macho yako

"yawe utepe katikati ya macho yako." Haya ni maneno badala ambayo uwakilisha mtu kuandika maneno ya Musa kwenye ngozi, kuweka ngozi kwenye mkoba, na kuifunga ili ikae kati ya macho yako. Mbadala huu unaweza kuwa mfano ambao unamaanisha mtu anapaswa kuwa mwangalifu kutii amri zote za Musa.

utepe

urembo mtu uvaa kwenye paji la uso

wakati unapoketi kwenye nyumba yako, wakati unapotembea njiani, wakati unapo lala chini, na wakati unapo nyanyuka.

Kutumia maeneo tofauti "kwenye nyumba" na "njiani," na kinyume "wakati unapo lala" na "kunyanyuka," uwakilisha popote, wakati wowote. Watu wa Israeli walipaswa kujadili amri za Mungu na kuzifundisha kwa watoto wao wakati wowote na popote.

Deuteronomy 11:20

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

kwamba siku zenu na siku za watoto wenu ziweze kuongezeka

Hapa "siku" uwakilisha muda mrefu wa wakati. Hii inaweza kutajwa kwa kauli tendaji. "ili kwamba Yahwe aweze kuwasababisha ninyi na watoto wenu kuishi muda mrefu"

kwa mababu zenu

Hii urejea kwa Abrahamu, Isaka, na Yakobo.

kuwapa maadamu mbingu ziko juu ya ardhi.

Hii ulinganisha kwa muda kiasi gani watu hawa wataweza kuishi katika nchi kwa muda kiasi anga litakuwepo juu ya ardhi. Hii ni njia ya kusema "milele"

Deuteronomy 11:22

Taarifa ya ujumla

Musa aendelea kuzungumza na wanaisraeli

Kama mtayashika kwa bidii maagizo haya yote ambayo ninawaamuru nyinyi, ili kwamba myafanye

"Kama mnakuwa makini kufanya kila kitu nilichokuamuru"

tembea katika njia zake zote

Namna gani Yahwe anahitaji mtu aishi na kutenda inazungumza kama walikuwa njia au barabara ya Yahwe. Mtu kumtii Yahwe kunasemwa kama alikuwa anatembea kwenye njia au barabara ya Yahwe.

kushikama naye

Kuwa na ushirika na Yahwe na kumtegemea yeye kunazungumza kama mtu anayeshikamana na Yahwe.

yote haya mataifa toka mbele yako,na utawafukuza mataifa

Hapa "mataifa" uwakilisha makundi ya watu tayari yanaishi huko Kanaani. "Yote haya makundi ya watu kutoka mbele yako, na utachukua ardhi kutoka makundi ya watu"

Kubwa na nguvu zaidi kuliko ninyi

Ingawa jeshi la Israeli ni dogo na dhaifu zaidi kuliko vikundi vya watu wanaoishi Kanaani, Yahwe atawawezesha watu wa Israeli kuwashinda.

Deuteronomy 11:24

Habari za jumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Kila mahali ambapo unyao wa mguu wako utaenda

Hapa "unyao wa mguu wako" uwakilisha mtu mzima.

kutoka kwenye mto, mto Euphrates

"kutoka kwenye mto Euphrates"

Hakuna mwanaume ataweza kusimama mbele yako.

Maneno "kusimama mbele yako" ni nahau. "hakuna mtu ataweza kukusimamisha" au "hakuna mtu ataweza kukupinga wewe"

Yahwe Mungu wako ataiweka hofu yako na hofu yako juu ya nchi yote unayoenda.

Yahwe anasababisha watu kuwa waoga sana inazungumwa kama kuogopa na hofu kilikuwa kitu ambacho ataweka juu ya watu.

kuogopa kwako na hofu yako

Maneno "kuogopa" na "hofu" umaanisha kitu kile kile na kusisitiza kiwango cha hofu.

juu ya nchi yote unayoiendea

Hapa "nchi" ni kielezo cha watu wote katika nchi.

Deuteronomy 11:26

Habari ya jumla

Hapa Musa afanya muhtasari wa chaguzi mbili za watu wa Israeli wanaweza kuchagua. Wanaweza kuchagua kumtii na kupokea baraka za Mungu au wanaweza kuchagua kutomtii na kupokea adhabu ya Mungu.

Tazama, naweka mbele yako leo baraka na laana.

Kuwapa watu chaguzi kama wao wanahitaji kubarikiwa au kulaaniwa huzungumzwa kwama baraka na laana ni vitu ambavyo Musa anaweka mbele yenu.

Baraka

Kitambulisho hiki kinaweza kutajwa kama kitenzi. "Mungu atawabariki ninyi"

laana

Kitambulisho hiki kinaweza kutajwa kama kitenzi. "Mungu atawalaani ninyi"

Lakini jiepushe na njia ambayo ninakuagiza leo, kufuata miungu mingine

Hizi amri za Yahwe ambazo Musa anawaambia watu huzungumzwa kama ilikuwa njia au barabara ya Mungu. Kutotii amri za Mungu husemwa kama mtu hugeuka kimwili mbali na Yahwe kufuata miungu mingine.

kufuata miungu mingine ambayo hujui

Maneno "miungu ambayo hujui" urejea kwa miungu ambayo makundi mengine uabudu. Waisraeli wanamjua Yahwe kwa sababu amejifunua mwenyewe kwao na wamepata uwezo wako.

Deuteronomy 11:29

Habari ya jumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

utaweka baraka juu ya mlima Gerizimu, na laana juu ya Mlima Ebali

Baraka na laana huzungumzwa kama vilikuwa vitu ambavyo mtu ataweka kwenye milima. "baadhi yenu wanapaswa kusimama juu ya Mlima wa Gerazimu na kutangaza nini kitakachomfanya Yahwe awabariki, and wengine wanapaswa kusimama juu ya Mlima wa Ebali na kutangaza nini kitamsababisha Yahwe kuwalaani"

Mlima Gerizimu...Mlima Ebali

Haya ni majina ya milima huko upande wa mashariki mwa mto Yordani.

Je, si zaidi ya Yordani..Moreh?

Waisraeli wkao upande wa mashariki mwa mto Yordai. Musa atumia swali kuwakumsha watu ambapo milima hii iko wapi. Swali hili linaweza kutajwa kama taarifa.

zaidi ya Yordani

"upande wa magharibi wa Mto Yordani"

magharibi ya barabra ya magharibi

"magharibi"

juu ya Gilgal

"karibu na Gilgal" Hii inaweza kuwa si sawa na mji karibu na Jeriko. Musa anaweza kuwa akimaanisha mahali karibu na Schechem.

Oaks ya Moreh

Hii ni miti takatifu karibu na Gilgali.

Deuteronomy 11:31

Habari ya jumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

amri zote na amri

Hizi ni amri na amri Musa atawapa katika Kumbukumbu la Torati 12-26

Ninaweka mbele yenu leo

Hii haina maana hizi ni mpya. Musa anatazama amri sawa na amri ambazo alitoa miaka 40 mapema.

Ninaweka mbele yenu

Amri za Mungu na amri, ambazo Musa anawaambia watu, huzungumzwa kama vilikuwa ambavyo Musa anaweka mbele ya watu.

Deuteronomy 12

Deuteronomy 12:1

Habari ya jumla

Musa bado anaongea na watu wa Israeli.

utazishika

"unapaswa kutii"

siku zote ambazo unaishi juu ya ardhi

Hapa "siku"uwakilisha muda mrefu zaidi. Pia, "kuishi juu ya ardhi" ni nahau ambayo inamaanisha muda mrefu mtu anaishi.

hakika utaangamiza

"Unapaswa kuangamiza"

mataifa utakayofukuza

Hapa "mataifa" uwakilisha makundi ya watu ambayo wanaishi huko Kanaani.

Deuteronomy 12:3

Habari ya jumla

Musa bado anazungumza na watu wa Israeli.

utavunja madhabahu zao

"lazima uondoe madhabahu ya mataifa hayo" au lazima uharibu madhabahu ya mataifa hayo"

vunja katika vipande vipande

"vunja vipande vipande au kupasua"

utakata chini

"unapaswa kukata"

haribu majina yao

Hapa "majina yao" uwakilisha "kumbukumbu zao.

mahali hapo

Hii urejea kwa kila eneo ambapo mataifa waliabudu miungu mingine.

Hutamwabudu Yahwe Mungu wako kama hivyo

"Haupaswi kumwabudu Yahwe Mungu wako kama vile haya matiafa mengine waliabudu miungu yao"

Deuteronomy 12:5

mahali ambapo Yahwe Mungu wako atachagua katika kabila zako zote ili kuweka jina lake

Hapa "jina lake" urejea kwa Mungu mwenyewe. Yahwe atachagua eneo moja ambako atakaa na watu watakuja kumwabudu huko.

ni huko mtaende

Wataenda kumwabudu ambako Mungu ameamua.

sadaka iliyotolewa kwa mkono wako

Hapa "mkono" uwakilisha mtu mzima.

"sadaka zako kwa ajili ya viapo, sadaka zako za uhuru

"sadaka zako hutimiza kiapo, sadaka zako za hiari. Hizi ni aina za sadaka.

mzaliwa wa kwanza wa ng'ombe zako na kondoo

Mungu anahitaji kwamba watu wampe kila mwanaume wa kwanza mazaliwa wa mifugo yao.

Deuteronomy 12:7

Ni pale

Hii urejea kwa eneo ambalo Yahwe atachagua kwa watoto wa Israeli kuabudu.

furahia juu ya kila kitu ambacho umeweka mkono wako

Hapa "umeweka mkono wako" uwakilisha mtu mzima na kazi aliyofanya.

Deuteronomy 12:8

Hauwezi kufanya mambo yote tunayofanya leo leo.

"Huwezzi kufanya kama tunavyofanya hapa leo." Hii ina maana kwamba wangeabudu katika nchi iliyoahidiwa tofauti na jinsi walivyokuwa wanaabudu wakati huo.

sasa kila mtu anafanya chochote kilicho sahihi machoni pake mwenyewe.

Hapa "machoni" uwakilisha mawazo ya mtu au maoni.

kwa wengine

Jina hili "kwa wengine" linaweza kutajwa kama tendo.

kwa urithi ambao Yahwe Mungu wenu anawapa ninyi

Nchi ambayo Mungu anawapa watu wa Israeli huzungumzwa kama miliki ambayo baba huacha kama urithi kwa watoto wake.

Deuteronomy 12:10

na kuishi katika nchi

Hii urejea kwa nchi ya Kanani.

katika nchi ambayo Yahwe Mungu anawasababisha kurithi

Mungu anawapa nchi ya Kanani kwa watu wa Israeli huzungumzwa kama walikuwa baba anawapa kama urithi watoto wake.

wakati anawapa ninyi pumziko toka maadui zenu wote waliowazunguka

wakati anawapa ninyi amani toka maadui zenu wote waliowazunguka"

kisha itakuwa kwamba kwa eneo ambalo Yahwe Mungu wenu atachagua kusababisha jina lake kuishi

Hapa "jina" uwakilisha Mungu mwenyewe.

sadaka iliyotolewa kwa mkono wako

Hapa "mkono" uwakilisha mtu mzima

matoleo yako yote ya kuchagua kwa ajili ya viapo

"sadaka zako zote za hiari ili kutimiza ahadi

Deuteronomy 12:12

Habari ya jumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

furahi mbele za Yahwe

"furahi katika uwepo wa Yahwe"

Walawi ambao wako ndani ya lango lako

Hapa " malango" kumbukumbu ya mji wenyewe.

kwa sababu hana sehemu au urithi miongoni mwenu

Ukweli kwamba Yahwe hawezi kutoa yoyote ya ardhi kwa Walawi huzungumzwa kama baba hakuwa anawapa urithi.

yeye hana sehemu

Hapa "yeye" urejea kwa Mlawi. Mlawi uwakilisha watoto wake

Deuteronomy 12:13

Habari ya jumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Jihadhari wewe mwenyewe

kuwa mwangalifu

kila eneo ambalo unaloliona

"eneo lolote ambalo linakubariki wewe" au " popote unataka"

lakini ni mahali ambapo Yahwe atachagua

Sadaka za kuteketeza zinapaswa kufanywa hekaluni. Yahwe mwenyewe atachagua wapi hekalu liwekwe.

Deuteronomy 12:15

Hata hivyo, unaweza kuua na kula nyama ndani ya milango yako yote

Watu wataweza peke kuua wanyama kama dhabihu katika eneo ambalo Yahwe atachagua. Wangeweza kuua wanyama kwa ajili ya chakula popote wangetaka. Maana kamili ya maelezo haya yanaweza kufanywa wazi.

ndani ya malango yako

Hapa "malango" uwakilisha mji wote.

si mfsafi...watu

Watu ambao hapokelewi kwa makusudi ya Mungu huzungumzwa kama mtu ambaye si msafi.

watu safi

Mtu ambaye anapokelewa kwa makusudi ya Mungu huzungumzwa kama mtu ambaye ni msafi.

kulungu na paa

Hawa ni wanyama wa mwitu wenye miguu mrefu mwembamba ambayo inaweza kukimbia haraka

Lakini hautakula damu

Damu uwakilisha maisha na Mungu hakuruhusu watu kula damu sambamba na nyama.

Deuteronomy 12:17

Habari ya jumla

Musa anaelezea kwa watu sadaka zote maalumu na dhabihu ambazo zinapaswa kufanywa hekaluni.

ndani ya malango

Hapa "malango" uwakilisha mji mzima.

wala ile ya sadaka uliyoitoa kwa mkono wako

Hapa "mkono" uwakilisha mtu mzima.

Deuteronomy 12:18

Habari ya jumla

Yahwe aendelea kuzungumza kwa watu wa Israeli.

utakula

"utakula sadaka zako"

mbele ya Yahwe

"katika uwepo wa Yahwe

Mlawi aliyeko ndani ya malango yako

Hapa "mlango" uwakilisha mji mzima.

kila kitu ambacho unaweka mkono wako

Hapa "kuweka mkono wako" uwakilisha mtu mzima na kazi ambayo umefanya.

Uwe makini mwenyewe

"uwe mwangalifu"

kwamba usiache

Hii inaweza kutajwa kwa kauli chanya

Deuteronomy 12:20

kuza mipaka yako

"kuza eneo lako" au "jipe eneo kubwa zaidi"

unasema, 'nitakula nyama; kwa sababu ya hamu ya kula nyama

hii ni nukuu ndani ya nukuu. Hii ni nukuu ya moja kwa moja inaweza kutajwa kama nukuu ya siyo ya moja kwa moja.

kama hamu za royo yako

Hapa "roho" urejea kwa mtu mzima

Deuteronomy 12:21

Habari ya jumla

Musa aendelea kuzungumza kwa watu wa Israeli.

anachagua kuweka jina lake

Hapa "jina" urejea kwa Mungu mwenyewe. Yahwe angeweza kuchagua eneo ambapo ataishi na watu watakuja kumwabudu yeye.

ndani ya malango yako

Hapa "malango" uwakilisha mji mzima

kama hamu ya nafsi yako

Hapa "nafsi" urejea kwa mtu mzima

Kama paa na kulungu wanaliwa

Hii inaweza kutofasiriwa kwa kauli tendaji.

paa na kulungu

Hawa ni wanyama wa mwituni mwenye miguu mirefu miembamba ambayo ukimbia kwa haraka.

asiye mfsafi...watu

Mtu asiyekubalika kwa kusudi la Mungu imesemwa kama mtu huyo alikuwa najisi kimwili.

watu safi

Mtu anayekubalika kwa kusudi la Mungu imesemwa kama mtu huyo alikuwa msafi kimwili.

Deuteronomy 12:23

damu ni uhai

hapa njia ambayo damu huimarisha uhai inazungumzwa kama kama damu ilikuwa maisha yenyewe.

hautakula maisha pamoja na nyama

Neno "maisha" hapa uwakilisha damu ambayo inaimarisha maisha.

kipi ni sawa machoni pa Yahwe

Hapa "macho" uwakilisha mawazo na maoni.

Deuteronomy 12:26

sadaka za viapo vyako

"sadaka kutimiza viapo" au "sadaka ya kiapo"

damu ya dhabihu zako itamwangwa nje

Hii inaweza kutajwa kwa kauli tendaji. "kuhani atamwanga damu ya dhabihu"

utakula nyama

Sheria ya Mungu inafafanua sehemu za mnyama ni za sadaka za kuteketezwa, ambayo sehemu ni za kuhani na ni sehemu gani za mtoaji.

Deuteronomy 12:28

Habari ya jumla

Musa aendelea kuzungumzwa kwa watu wa Israeli.

Chungunza na kusikiliza kwa maneno haya ambayo ninakuamuru

Hapa "maneno" uwakilisha nini Musa anasema.

ili iweze kukufanya vizuri wewe na watoto wako baada yako

Hapa "watoto" umaanisha watoto wako wote.

wakati unafanya kile kizuri na sawa

Maneno "uzuri" na "sawa" yana maana ya kufanana na msisitizo wa umuhimu wa tabia nzuri.

katika macho ya Yahwe

Hapa "macho" uwakilisha mawazo na maoni

Deuteronomy 12:29

hukataa mataifa

Yahwe kuwaharibu makundi ya watu huko Kanani huzungumza kama alikuwa akiwakata, kama mmoja angeweza kukata kwa vipande ngua au kukata tawi toka kwenye mti.

mataifa

Hapa "mataifa" uwakilisha watu kuishi huko Kanani.

wakati unapoenda kuwaondoa, na kuwaondoa

"wakati mnachukua vyote toka kwao"

uwa makini mwenywe

"uwe mwangalifu"

kwamba hujaingizwa katika kufuata...waliingia ndani ya kuchunguza miungu yao, kuuliza

Mtu kujifunza kuhusu na kuabudu miungu mingine huzungumzwa kama wameshikwa mtego wa mawindo. Hii inaweza kutajwa kwa kauli tendaji.

si kuingizwa ndani ya kufuata

Waisraeli kuabudu sanamu kama makundi ya watu Kanani kuabudu sanamu huzungumzwa kama Waisraeli walikuwa wanafuata nyuma ya makundi mengine ya watu.

baada ya kuharibiwa toka mbele yako

Hii inaweza kutajwa kwa kauli tendaji. "baada Yahwe awaharibu mbele yako"

katika kuuliza, "mataifa haya yanaabudu miungu yao? nitafanya hivyo'

Hii nukuu ndani ya nukuu. Nukuu ya moja kwa moja inaweza kutajwa kama nukuu ambayo si ya moja kwa moja.

Deuteronomy 12:31

Usiongeze au usiondoe

Hawapaswi kutengeneza sheria zaidi wala hawapaswi kupuuzia sheria ambazo Mungu amewapa.

Deuteronomy 13

Deuteronomy 13:1

Habari ya jumla

Musa aendelea kuzungumza kwa watu wa Israeli.

Ikiwa inainuka kati yenu

"Ikiwa inatokea miongoni mwenu" au "Ikiwa mmoja miongonu mwenu anadai kuwa"

mwotaji wa ndoto

Huyu ni yeyote ambaye anapokea ujumbe toka kwa Mungu kupitia ndoto.

ishara au maajabu

Haya ni maneno mawili yaliyo na maana ya kufanana na urejea kwa miujiza tofauti.

inakuja kuhusu

"inafanyika" au "hutokea"

ambayo alikuambia na akasema, 'hebu tufuate miungu mingine ambayo hamjui na tuiabudu.

Hii inaweza kutofasiriwa kama nukuu isiyo ya moja kwa moja.

Hebu tufuate miungu mingine.

Kuabudu miungu mingine huzungumzwa kama walikuwa wanaifuata au kufuata miungu mingine.

kufuata miungu mingine, ambayo hamjaijua

Maneno "miungu, ambayo hamjaijua" urejea kwa miungu ambayo makundi mengine ya watu kuabudu. Waisraeli wamjua Yahwe kwa sababu amejifunua mwenyewe kwao na wamepata udhoefu wa nguvu zake.

usisikilize maneno ya nabii, wala ya mwotaji wa ndoto

Hapa "maneno" uwakilisha kilichosemwa.

kwa moyo wako wote na roho yako yote

Hii ni nahau "kwa moyo wako wote" inamaanisha "kabisa" na "kwa ...roho" inamaanisha "kwa uzima wako wote. Haya maneno yana maana ileile.

Deuteronomy 13:4

Utakwenda kumfuata Yahwe Mungu wako

Kumtii na kumwabudu Yahwe huzungumzwa kama watu walikuwa wanatembea au kumfuata Yahwe.

tii sauti yake

Hapa 'sauti' uwakilisha nini Yahwe asema.

kuambatana naye

Kuwa na mahusiano mazuri pamoja na Yahwe na kabisa kumtegemea huzungumzwa kama mtu ameshikamana kwa Yahwe.

utauawa

Hii inaweza kutajwa kwa kauli kazi

amezungumza uasi

Jina "uasi" linaweza kutajwa kama kitenzi

aliyekukomboa katika nyumba ya utumwa

Yahwe kuokoa watu wa Israeli toka utumwa huko Misri huzungumzwa kama Yahwe alilipa pesa kuwaokoa watu wako toka utumwani.

nyumba ya utumwa

Hapa "nyumba ya utumwa" uwakilisha Misri ambapo watu wa Yahwe walikuwa watumwa.

kukuchochea njia ambayo Yahwe Mungu wako alikuamuru uende.

Jinsi Mungu anataka mtu kuishi au kuzungumwa kama kama njia au barabara ambalo Mungu wake watembee. Mtu anayejaribu kumfanya mtu mwingine ache kumtii Mungu huzungumzwa kama mtu huyo alikuwa anajaribu kumfanya mtu mwingine aende njia ya Mungu au barabara.

Basi weka mbali uovu mbali miongoni mwenu

Hapa "uovu" urejea kwa mtu muovu au tabia mbaya. Hili jina kivumushi linaweza kutajwa kama kivumishi. "Unapaswa kumwondoa miongoni mwa watu wa Israeli mtu anayefanya kitu kiovu" au " Unapaswa kumuuwa mtu huyu muovu"

Deuteronomy 13:6

Habari ya jumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

mke wa kifua chako

Kifua ni kifua cha mtu. Hii ni nahau ambayo anashikilia karibu na kifua chake, ambayo inamaanisha anampenda na kumthamini.

rafiki ambaye kwako ni kama nafsi yako

Hapa "nafsi" uwakilisha maisha ya mtu. Hii ina maana mtu anamjali rafiki wake zaidi kama anavyojali maisha yake mwenye.

kwa siri hukushawishi na kusema, hebu tuende na kuabudu mwisho mwingine wa dunia

Hii inaweza kutofasiriwa kama nukuu isiyo ya moja kwa moja. "kwa siri ujaribu kukushawishi uende na kuabudu... mwisho mwingine wa dunia."

ambayo ni pande zote karibu nawe

ambayo ni karibu nawe

kutoka mwisho wa dunia mpaka mwisho mwingine wa dunia

Hii ni kumbukumbu ya kutaja juu ya mambo makuu mawili ya dunia inamaanisha kila mahali duniani.

Deuteronomy 13:8

usimkubali

"Usikukabali kwa kile anataka "

Wala jicho lako lisimhurumie

Hapa "jicho lako" urejea kwa mtu mzima.

wala hautamzuia au kumficha

"wala hautamuonyesha huruma au kujificha kutoka kwa wengine kile alichokifanya"

mkono wako utakuwa wa kwanza kumuawa

Hii inamaanisha kwamba alikuwa wa kutupa jiwe la kwanza kwa mtu aliye na hatia. Neno "mkono" uwakilisha mtu mzima.

mkono wa watu wote

Hapa "mkono" uwakilisha mtu mzima. "watu wengine wataungana nawe"

Deuteronomy 13:10

amejaribu kukuchochea kutoka kwa Yahwe

"kugeuka mbali toka kwa Yahwe." Mtu anajaribu kusababisha mtu mwingine ache kumtii Yahwe husemwa kama mtu alikuwa anajaribu kumsababisha mtu kimwili kugeuka na kumwacha Yahwe.

nje na nyumba ya utumwa

Hapa "nyumba ya utumwa" uwakilisha Misri ambapo watu wa Yahwe walikuwa watumwa.

Israeli yote atasikia na kuogopa

Ilimaanisha kwamba wakati watu wanasikia kuhusu mtu aliyeuawa, watakuwa na hofu ya kutenda kama alivyofanya.

Deuteronomy 13:12

Habari ya jumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Wenzake wengine waovu wamekwenda kati yenu

Maneno haya "kati yenu" umaanisha kwamba wanaume hawa waovu walikuwa Waisraeli walioishi kwenye jamii zao.

wamewaondoa wenyeji wa jiji lao na kusema tuache na kuabudu miungu mingine ambayo hamjui

Hii inaweza kutofasiriwa kama nukuu isiyo ya moja kwa moja.

amewaondoa wenyeji mbali na mji wao

Mtu anasababisha mtu mwingine kuacha kumtii Yahwe husemwa kama mtu aliyemsababisha mtu mwingine kimwili kugeuka na kumwacha Yahwe

kuchunguza ushahidi, kufanya utafutaji, na kuchunguza vizuri

Haya maneno yote umaanisha kimsingi kitu kilekile. Musa anasisitiza kwamba wanapaswa kwa umakini kujua nini kilichotokea kweli katika mji

kwamba kitu hicho cha machukizo kimefanyika kati yenu

Hii inaweza kutajwa kwa kauli tendaji. "kwamba watu wa mji wamefanya kitu kibaya"

Deuteronomy 13:15

kwa makali ya upanga

Hapa "makali" uwakilisha upanga mzima.

nyara zote

"nyara zote." Hii urejea kwa milki na hazina ambazo jeshi linakusanya baada ya kushinda vita

chungu cha uharibifu

"rundo la uharibifu"

kwamwe isijengwe tena

Hii inaweza kutajwa kwa kauli tendaji. "hakuna mmoja anapaswa kujenga mji huu"

Deuteronomy 13:17

Hakuna vitu vilivyotengwa kwa ajili ya uharibifu lazima viingie mkononi mwako

Yahwe alaani kitu fulani na kuahidi kukiharibu husemwa kama Yahwe alikuwa anaweka kitu mbali na vitu vingine. Hii inaweza kutajwa kwa kauli tendaji.

lazima viingine mkononi mwako

Hii ni nahau. "Unapaswa kuishika"

Yahwe atageuka kutoka kwa hasira yake kali

Yahwe hana hasira tana inaelezewa kuwa hasira yake ilikuwa kitu na Yahwe kimwili anageuka mbali nayo"

kwa baba zako

Hapa "baba" umaanisha babu ua baba waliotangulia.

unasikiliza sauti ya Yahwe

Hapa "sauti" uwakilisha nini Yahwe asema. "unatii kile Yahwe asema"

ambacho ni sahihi machoni pa Yahwe Mungu wenu

Hapa "machoni" uwakilisha mawazo au maoni.

Deuteronomy 14

Deuteronomy 14:1

Habari ya jumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Ninyi ni watu...ninyi ni taifa...amewachagua

tukio lote la "wewe" urejea kwa watu wa Israeli. Musa alijumuishwa kama sehemu ya watu.

Msijivunue, wala msiweke sehemu yoyote ya uso wako kwa wafu

Hizi zilikuwa njia za makundi ya watu waishio Kanani walionyesha kwamba walikuwa wakihuzunika juu ya watu walio kufa. Musa anawambia watu wa Israeli wasifanya kama wao. Maana kamili ya maelezo haya inaweza kuwa wazi.

wala kunyoa sehemu ya uso wao

"wala kunyoa mbele ya kichwa chako"

wewe ni taifa ambalo limetengwa kwa Yahwe Mungu wako.

Yahwe anachagua watu wa Israeli kuwa wake katika njia maalumu husemwa kama Yahwe aliwatenga kutoka mataifa mengine yote.

Yahwe amewachagua ninyi kuwa watu kwa ajili ya miliki yake.

Hii humaanisha kimsingi kitu kile kama sehemu ya kwanza ya sentensi. Vyote humaanisha watu wa Israeli kuwa sehemu ya Yahwe kwa njia maalumu.

watu kwa ajili ya miliki yake

"watu kwa ajili ya miliki ya hazina" au "watu wake"

zaidi ya watu wote ambao wako juu wa uso wa ardhi.

nje ya makundi wa watu katika ulimwengu.

Deuteronomy 14:3

Haupaswi kula kitu chochote chukizo

Watu wa Israeli hakuwapaswa kula kitu chochote ambacho Mungu alisema hakikua kizuri kwa kuliwa.

paa, kulungu na kulungu wa kiume

Hizi ni aina za paa. Kama katika lugha yako hauna neno kwa kila mnyama inaweza kutofasiriwa kama "aina yote ya paa"

Kulungu

Huyu ni mnyama wa mwituni akiwa na miguu mirefu mwembamba ambayo inaweza kukumbia kwa haraka.

Kulungu wa kiume

aina ya paa

bebe, na swala

Wote hawa ni aina ya swala. Kama lugha yako haina neno kwa ajili ya mnyama inaweza kutofasiriwa kama "aina yote ya swala."

Deuteronomy 14:6

sehemu hiyo ya kwato

"ambayo wamegawanyika kwato" Hii ni kwato ambayo imegawanyika katika sehemu mbili badala ya kuwa moja kamili.

utafuna macheuo

Hii umaanisha wanyama uleta chakula chake juu toka tumboni na kutafuna tena.

sungura

Huyu ni mnyama mdogo mwenye masikio marefu ambaye huishi kwenye mashimu ya ardhi.

pomono

Huyu ni mnyama mdogo ambaye huishi kwenye maeneo ya miamba.

wako najisi kwenu

Kitu chochote Yahwe usema hakifai kwa watu wake kula husemwa kama kilikuwa najisi kimwili.

Deuteronomy 14:8

Nguruwe ni najisi kwenu

Kitu chochote Yahwe usema hakifai kwa watu wake kula husemwa kama kilikuwa najisi kimwili.

Deuteronomy 14:9

Habari ya jumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Kwa vitu hivi ambavyo viko kwenye maji mnaweza kula

"Mnaweza kula aina hii ya wanyama ambayo huishia kwenye maji"

mapesi

mapesi, sehemu tambarare ambayo samaki hutumia kwenda kupitia maji

magamba

sahani ndogo zinazofunika mwili wa samaki

wao ni najisi kwa ajili yenu

Kitu Yahwe usema hakifai kwa ajili ya watu wake kula husemwa kama kilikuwa najisi kimwili.

Deuteronomy 14:11

ndege wote safi

Mnyama ambaye Mungu usema anafaa kwa ajili ya watu wake kula husemwa kama mnyama aliye msafi kimwili.

tai...tumbusi...kipungu...mwewe mwekundu na mweusi...kipanga.

Hizi ni ndege ambazo zinaweza kuamka usiku au kula wanyama wadogo na wanyama waliokufa.

Deuteronomy 14:14

kunguru...mnandio

Hizi ni aina yote ya ndege ambao wanaweza kuamka usiku au kula wanyama wadogo na wanyama waliokufa.

Deuteronomy 14:18

korongo...kongoti, hudihudi

Hizi ni aina za ndege ambao hula wanyama wadogo na mijusi.

popo

mnyama aliye na mabawa na mwili wa manyoya ambao umeamka hasa usiku na hula wadudu na panya.

vitu vyote vilivyo na mabawa, vyema

Hii umaanisha wadudu wote warukao ambao utembea kwa makundi makubwa.

wao ni najisi kwenu

Wanyama ambao Mungu usema hawafai kwa ajili ya watu wake kula husemwa kama wanyama walio najisi kimwili.

hawapaswi kuliwa

Hii inaweza kutajwa kwa kauli tendaji. "haupaswi kuwala"

vitu vyote visafi virukavyo

Wanyama ambayo Mungu husema wanafaa kwa ajili ya watu wake kula husemwa kama wanyama walio safi kimwili.

Deuteronomy 14:21

Habari ya jumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli

kitu chochote ambacho hufa chenyewe

Hii ina maanisha mnyama ambaye hufa kwa kifo cha kawaida.

Kwa kawa u taifa ambalo limewekwa wakfu kwa Yahwe Mungu wenu.

Yahwe kuchagua watu wa Israeli kuwa ni wake kwa anjia maalumu husemwa kama Yahwe amewatenga toka mataifa mengine.

Deuteronomy 14:22

toa sehemu ya kum ya mazaoa ya mbegu yako

Hii umaanisha wanapaswa kutoa moja ya sehemu nje ya kila kumi sawa na sehemu toka mazaoa yao.

miaka baada ya miaka

"kila mwaka"

mbele ya Yahwe

"kwenye uwepo wa Yahwe"

Deuteronomy 14:24

ibebbe

Hapa "i" urejea kwa kumi ya mazao na mifugo.

utabadilisha sadaka kwa fedha

"utauza sadaka yako kwa fedha"

funga fedha katika mkono wako, uende

"weka fedha kwenye mkoba na uchukue pamoja nawe"

Deuteronomy 14:26

kwa chochote utamanicho

"kwa chochote unataka"

mbele ya Yahwe

"kwenye uwepo wa Yahwe"

Mlawi aliye ndani ya malango yako

Hapa "lango" uwakilisha mji wote.

usimsahau yeye

Hii inaweza kutajwa kwa kauli chanya. "hakikisha unatoa moja ya kumi yako kwa Mlawi"

kwa kawa hana sehemu wala urithi pamoja nawe

Kabila la Lawi halikupokea sehemu ya ardhi kama urithi. Mgao wao wa urithi ulikuwa heshima ya kumtumikia Yahwe kama makuhani wake. Maana kamili ya maelezo haya inaweza kuwafanywa wazi.

hakuna sehemu wala urithi pamoja nawe

Mungu hakutoa ardhi kwa Walawi husemwa kama hakuwapa urithi.

Deuteronomy 14:28

kila baada miaka mitatu utawasilisha sehemu ya kumi ya mazao yako

Mara moja kwa kila miaka mitatu Waisraeli walipaswa kutunza moja ya kumi zao ndani ya miji yao ingetumika kutoa kwa Walawi, yatima, wajane na wageni.

ndani ya malango yenu

Hapa "malango" uwakilisha mji wote

kwa sababu hana sehemu wala urithi pamoja nawe

Mungu hawapi ardhi yoyote Walawi husemwa kama hakuwapa urithi.

yatima

Hawa ni watoto ambao wazazi wao wote wamekufa na hawana ndugu wa kuwajali.

mjane

Huyu ni mwanamke ambaye mme wake amekwisha kufa na hana watoto wa kumjali katika umri wake wa uzee.

kwa kazi yote mkon wako ambayo unafanya.

Hapa "mkono" uwakilisha mtu mzima. HIi inaweza kurejea kwa kazi ya mtu hufanya.

Deuteronomy 15

Deuteronomy 15:1

Habari ya jumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

miaka saba

"miaka 7"

unapaswa kufuta madeni

"msamehe kila kitu ambacho watu bado wanadaiwa"

Hii ndiyo njia ya kutolewa

"Hii ni namna ya kufuta madeni"

mkopaji

mtu anayekopesha watu wengine fedha.

jirani yake au ndugu yake

Maneno "jirani" na "ndugu" kushiriki maana zilezile na msisitizo wa uhusiano wa karibu ambao wana nao na Waisraeli wenzake.

kwa sababu kufuta kwa madeni ya Yahwe kumetangazwa

Hii inaweza kutajwa kwa kauli tendaji. "kwa sababu Yahwe amehitaji kwamba kufutwe madeni"

mkono wako unapaswa kutolewa

Hii ni nahau. "unapaswa kudai tena" au " unapaswa ulipaji"

Deuteronomy 15:4

hakuna masikini

Kitenzi cha jina "masikini" kinaweza kutajwa kama kitenzi. "hakuna watu masikini" au "hakuna mmoja ambaye ni masikini"

ardhi ambayo ametoa

Hii urejea kwa nchi ya Kanani.

anawapa ninyi kama urithi wa kumiliki

Nchi ambayo Yahwe anawapa watu wake husemwa kama ilikuwa ni urithi ambao Yahwe anawapa.

kama peke kwa bidii unasikiliza sauti ya Yahwe Mungu wako

Hapa maneno "sauti ya Yahwe" urejea kwa kile Yahwe mwenyewe asema. "kama peke unakuwa mwangalifu kutii kile Yahwe Mungu wako anasema"

utakopesha mikopo...huwezi kukopa

Neno "pesa" linaeleweka. Unaweza kufanya maana kamili ya maelezo haya wazi.

kwa mataifa mengi...juu ya mataifa mengi

Hapa "mataifa" uwakilisha watu. "kwa watu wa mataifa mengi...juu ya watu wa mataifa mengi"

utaongoza juu ya mataifa mengi, lakini hawatawaongoza juu yenu

Hapa "juu yenu" umaanisha kuwa mkuu wa kifedha. Hii umaanisha kimsingi kitu kile kama sehemu ya awali ya sentensi.

Deuteronomy 15:7

Kama kuna mtu maskini

Hapa "mtu" umaanisha mtu kwa ujumla.

moja wa ndugu zenu

"mmoja wa Waisraeli wenzako"

ndani ya malango yako

Hapa "malango" uwakilisha mji mzima.

haupaswi kuufanya mgumu moyo wako

Kuwa mkaidi husemwa kama mtu huyo alifanya mgumu moyo wao.

wala usifungi mkono wako kutoa kwa ndugu yako masikini.

Mtu ambaye akataa kuto kwa mtu maskini husemwa kama anafunga mkono wake kwamba mtu masikini hawezi kupata chochote toka kwake.

lakini unapaswa kwa uhakika kuufungua mkono wako kwake

Mtu anamsaidia mtu masikini husemwa kama alifungua mkono wake kwake.

Deuteronomy 15:9

hapana kuwa na mawazo maovu ndani ya moyo wako, kusema

Hapa "moyo" uwakilisha akili ya mtu. "usifikiri mawazi maovu"

Mwaka wa saba, mwaka wa kutolewa, u karibu

Ina maana kuwa kwa haraka mtu anafikiria hii atakuwa na wasiwasi kumsaidia mtu maskini kwa sababu inawezekana kwamba mtu maskini hatastahili kulipa tena. Maana kamili ya maelezo haya inaweza kufanywa wazi.

Mwaka wa saba

Neno "saba" ni namba ya upeo ya saba.

mwaka wa kutolewa

"mwaka wa kufuta madeni"

u karibu

Kitu fulani kitatokea mapema husemwa kama kilikuwa karibu kimwili.

ili usiwe na uchungu juu ya ndugu yako maskini na usimpe kitu

"ili usije ukaidi na kukataa kutoa chochote kwa Waisraeli wenzako"

lila kwa Yahwe

"piga kelele kwa Yahwe kwa ajili ya msaada"

itkauwa dhambi kwako

"Yahwe atachunguza yale uliyoyatenda kuwa ya dhambi

moyo wako lazima usiwe na huruma

Hapa "moyo" uwakilisha mtu mzima

katika yote ambayo unaweka mkono wako

Hapa "kuweka mkono wako" uwakilisha mtu mzima na kazi ambazo amefanya.

Deuteronomy 15:11

Kwa kuwa masikini kamwe wataacha kuishi kwenye nchi

Hii inaweza kutajwa kwa mfumo chanya. "Kwa kuwa daima kutakuwa na watu maskini katika nchi"

kwa masikini

Jina kitenzi "maskini" linaweza kutajwa kama kitenzi.

Nakuamuru na kusema, "Unapaswa hakika kufungua mkono wako...kwenye nchi yako.'

Hii ina nukuu ndani ya nukuu. Nukuu ya moja kwa moja inaweza kutajwa kama nukuu isiyo ya moja kwa moja.

fungua mkono wako kwa ndugu yako, kwa mhitaji, na masikini wako

Mtu ambaye ana utayari kumsaidia mtu mwingine husemwa kama mkono wake uko wazi.

ndugu yako, kwa mhitaji wako, na masikini wako

Maneno "mhitaji" na "masikini" umaanisha kimsingi kitu kile kile na kusisitiza kwamba hawa ni watu ambao hawezi kujisaidia wenyewe.

Deuteronomy 15:12

Habari ya jumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Kama ndugu yako

Hapa "ndugu" umaanisha Mwisraeli kwa ujumla, kama ni mwanaume au mwanamke.

imeuzwa kwako

Kama watu wasingeweza kulipa madeni, kwa wakati mwingine wanajiuza wenyewe kwa biashara ya utumwa kuplipa kile walichodaiwa.

miaka sita

"miaka 6"

mwaka wa saba

"mwaka wa saba." Huu "mwaka wa sabab ni namba ya upeo ya saba.

usiruhu aende zako mkono tupu

Mtu ambaye hana mali ya kujitolea mwenyewe au familia yake inazungumzwa kama kama mikono yake ilikuwa tupu.

kutoa kwa hiari

"hiari utoa kwake"

Deuteronomy 15:15

kumbuka ulikuwa mtumwa

Hapa "u" inajumuisha babu ambao walikuwa watumwa kwa miaka mingi.

kwamba Yahwe Mungu wenu aliwakomboa

Yahwe kuwaokoa watu wa Israeli kutoka utumwa huko Misri husemwa kama Yahwe alilipa pesa kuwaokoa watu wake kutoka utumwani.

kama anasema kwenu, "Sitaenda mbali nanyi"

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. Nukuu ya moja kwa moja inaweza kutajwa kama nukuu isiyo ya moja kwa moja.

nyumba yako

Hapa "nyumba" uwakilisha familia ya mtu.

basi unapaswa kuchukua uma na kuifanya kupitia sikio lake kwa mlango

"basi utaweka mkono wako karibu na fremu ya mlango wa mbao kwenye nyumba yako, na kisha weka fikra za uma kupitia sikio ndani ya kuni"

uma

kikali, kifaa chenye ncha utumiwa kufanya shimo

milele

"mpaka mwisho wa maisha yake" au "mpaka afe"

Deuteronomy 15:18

Haipaswi kuonekana ngume kwenu kumruhusu yeye aende huru toka kwenu

Hii ina maana kwamba hawapendi wakati wa kuruhusu mtu aende huru.

kupewa mara mbili thamani ya mtu aliyeajiriwa

Hii ina maana mmiliki peke alipaswa kulipa ana kiasi kwa ajili ya mtumwa huyu kufanya kazi kuliko angemwajiri mtu kufanya kazi.

mtu kuajiriwa

Huyu ni mtu anayefanya kazi kwa malipo.

Deuteronomy 15:19

Habari ya jumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

kumnyoa

kukata pamba au nywele

mbele ya Yahwe

"kwenye uwepo wa Yahwe"

mwaka kwa mwaka

"kila mwaka" au "kila mwaka"

kipofu

walemavu au asiyejiweza kimwili.

Deuteronomy 15:22

ndani ya malango

Hapa "malango" uwakilisha mji mzima.

najisi... watu

Mtu ambaye hakubaliki kwa makusudi ya Mungu husemwa kama mtu najisi kimwili.

watu wasafi

Mtu ambaye anakubalika kwa makusudi ya Mungu husemwa kama mtu msafi kimwili.

paa na kulungu

Hawa ni wanyama wa mwitu wakiwa na miguu mirefu na mwembamba ambao hukimbia kwa haraka.

haupaswi kula damu yake

"haupaswi kula damu yake." Yahwe hakuwaruhusu waisraeli kula damu kwa sababu damu iliwakilisha uhai.

Deuteronomy 16

Deuteronomy 16:1

Habari ya jumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

mwezi wa Abibu

Huu ni mwezi wa kwanzza wa kalenda ya Kiebrania. Inaonyesha wakati Mungu aliwatoa watu wa Israeli toka Misri. Ni wakati wa sehemu ya mwisho wa mwezi wa tatu na sehemu ya kwanza ya mwezi wa nne kwa kalenda ya Magharibi.

ishike pasaka

Inamaanisha kwa "kushika pasaka" ambayo walikuwa wanasherehekea na kula chakula cha pasaka.

utatoa dhabihu ya pasaka

Hapa "Pasaka" uwakilisha mnyama ambaye anatolewa dhabihu kwa ajili ya sherehe.

Deuteronomy 16:3

nayo

Hapa "nayo" urejea kwa mnyama atakayetolewa dhabihu na kuliwa.

siku saba

"siku 7"

mkate wa taabu

Hii ilikuwa jina la mkate usiotiwa chachu.Maana kamili inaweza kutajwa kwa waziwazi.

nje ya ardhi ya Misri kwa haraka

Watu walipaswa kuondoka Misri kwa haraka ambako hakuwa na muda wa kutosha kufanya mkate wa amila.

Fanya hili kwa siku zote za maisha yako

"Fanya hili kwa muda mrefu unapoishi"

kumbuka akilini

Hii ni nahau. "kumbuka"

Hakuna chachu lazima ionekane kati yenu

Hii inaweza kutajwa kwa mfumo tendaji. "Haupaswi kuwa na chachu yoyote miongoni mwenu"

ndani ya mipaka yenu

"ndani ya wilaya yako yote" au "katika nchi yako yote"

siku ya kwanza

Hii "kwanza" ni namba ya upeo kwa moja.

Deuteronomy 16:5

Huwezi kutoa dhabihu Pasaka

Hapa "Pasaka" uwakilisha mnyama ambaye atatolewa dhabihu.

ndani ya milango yako yote ya jiji

Hapa "milango" uwakilisha miji

wakati wa jua kwenda chini

"wakati wa jua kwenda chini"

Deuteronomy 16:7

lazima uipike

"Unapaswa kuipika"

siku sita

"siku 6"

siku ya saba

"saba" ni namba ya upeo kwa saba

mkusanyiko mzuri

"mkusanyiko maalumu"

Deuteronomy 16:9

Habari ya jumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

hesabu wiki saba

"hesabu wiki 7"

tangu wakati unapoanza kuweka sungura kwenye nafaka zilizosimama.

Haya maneno "kuweka mundu kwenye nafaka" ni njia ya kurejea mwanzo wa muda wa kuvuna.

mundu

ni kifaa kilicho na wembe iliyopigwa kwa kukata nyasi, nafaka, na mizabibu.

pamoja na mchango wa sadaka ya kujitolea kutoka kwa mkono wako ambao utakupa

Hapa "mkono" uwakilisha mtu mzima.

kulingana na Yahwe Mungu wako amekubariki

"kulingana na mavuno ambayo Yahwe Mungu amekupa" Hii inamaanisha kwamba watu itatokana na kiasi ambacho wanatoa juu ya kiasi gani walichovuna mwaka huo.

Deuteronomy 16:11

mwana wako, binti yako, mjakazi wako wa kiume, mjakazi wako wa kike, Mlawi

Hawa hawarejei kwa mtu maalumu. Ina maana hawa ni aina ya watu kwa jumla.

ndani ya malango yako

Hapa "malango" uwakilisha miji

mgeni, yatima na mjane

Hii urejea kwa aina ya watu hawa kwa jumla

yatima

Hawa ni watoto ambao wazazi wao wote walifuga na hawana ndugu wa kuwajali.

mjane

Hii ina maana ya mwanamke ambaye mme wake amekufa na hana watoto wa kumjali kwa umri wa uzeeni.

kumbuka akilini

Hii ni nahau. "kumbuka"

Deuteronomy 16:13

Sherehe ya vipanda

Majina mengine ya sherehe ni "Sikukuu ya mahema," Sherehe ya vibanda," na "Sikukuu ya kukusanya." Wakati wa mavuno, wakulima wanategeneza vibanda vya muda kwenye mashamba. Hii sikukuu ilifanyika baada ya mavuno ya mwisho wa mwaka.

siku saba

"siku 7"

ndani ya malango

Hapa neno "malango" uwakilisha miji au mji.

Deuteronomy 16:15

sikukuu

"sikukuu ya vibanda"

kazi yote ya mikono yenu

Hapa "mikono" uwakilisha mtu mzima.

Deuteronomy 16:16

wanaume wote wanapaswa kuonekana mbele ya Yahwe

Wanawake waliruhusiwa, lakini Yahwe hakuwahitaji kwamba waje. Wanaume wangeweza kuwakilisha familia zao zote.

wanapaswa kuonekana mbele ya Yahwe

"wanapaswa kuja na kusimama kwenye uwepo wa Yahwe"

hawataonekana mbele ya Yahwe mikono mitupu; badala yake, kila mtu

mitupu; badala yake, kila mtu- hawatakuja mbele ya Yahwe bila kuwa na sadaka; badala yake, kila mtu." Hizi sentensi mbili hasi kwa pamoja zina maana chanya.

Deuteronomy 16:18

Habari ya jumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Mnapaswa kuwa na majaji

"Mnapaswa kuteua majaji" au " Mnapaswa kuchagua majaji"

ndani ya malango ya mji wenu

Hapa "malango" uwakilisha mji. "ndani ya miji yenu yote"

watachukuliwa

Hii inaweza kusemwa kwa mfumo tendaji. "utawachagua"

wahukumu watu kwa hukumu ya haki

"hukumu watu kwa haki"

Usiondoe haki kwa nguvu

Musa azungumzia haki kama kilikuwa kitu halisi ambacho mtu mwenye nguvu anaweza kwa ukali kutoa kwa mtu dhaifu. "Haupaswi kuwa na upendeleo wakati unahukumu. Hii inaweza kusemwa kwa mfumo chanya. Lugha yako inaweza kuwa na neno moja ambalo lina maanisha "tumia nguvu kuondoa." "Unapaswa kufanya maamuzi ya haki"

hampaswi

Hapa "m" urejea kwa wale watateuliwa kama majaji na maafisa.

kwa kuwa rusha upofusha macho ya hekima na kupotosha maneno ya wenye haki

Kuchukua rusha husemwa kama rushwa uwaharibu watu. "kwa kuwa hata mtu wa hekima ambaye apokea rushwa atakuwa kipofu, na hata mtu mwenye haki apokea rushwa atasema uongo"

rushwa upofusha macho ya mwenye hekima

Mtu wa hekima apokeae rushwa ili asiongee dhidi ya kitu kiovu husemwa kama amekuwa kipofu.

mwenye hekima

Kivumishi jina "mwenye hekima" kinaweza kutofasiriwa kama kivumishi.

na kupotoshwa maneno ya mwenye haki

Kivumishi jina "haki" kinaweza kutofasiriwa kama kivumishi.

kufuata baada ya haki, baada ya haki pekee

haki husemwa kama mtu ambaye anatembea. Mtu ambaye anafanya kile kilicho sawa na haki husemwa kama alikuwa anafuta kwa karibu nyuma ya haki.

urithi nchi ambayo Yahwe Mungu wenu anawapa

Kupokea nchi ambayo Mungu anawapa watu husemwa kama watu walikuwa wanarithi nchi kutoka kwa Mungu.

Deuteronomy 16:21

hampaswi

Hapa "m" urejea kwa watu wote wa Israeli.

nguzo yoyote ya jiwe takatifu, ambayo Yahwe Mungu wako huchukia.

Maneno "ambayo Yahwe Mungu wako huchukia" inakupa taarifa zaidi kuhusu jiwe takatifu.

nguzo ya jiwe takatifu

Hii urejea kwa nguzo ambazo ni sanamu hutumiwa kuabudu miungu wa uongo.

Deuteronomy 17

Deuteronomy 17:1

Habari ya jumla

Musa bado anazungumza na watu wa Israeli.

ambayo ni kosa lolote

"ambayo ina kosa" au "ambayo ina kitu kibaya" Mnyama anapaswa kuonekana mwenye afya pasipo kuwa na ulemavu.

hiyo itakuwa chukizo kwa Yahwe

"ambayo itakuwa machukizo kwa Yahwe"

Deuteronomy 17:2

kama kunapatikana miongoni mwenu

Hii inaweza kusemwa kwa kauli tendaji. "Kama unampata mtu" au "Kama kuna mtu yeyote miongoni mwenu"

ndani ya malango ya mji wenu wowote

Hapa "malango" uwakilisha miji. "kuishi kwenye moja ya miji yenu"

Je, ni jambo baya machoni pa Yahwe Mungu wako

Hapa, "machoni pa Yahwe" umaanisha nini Yahwe azingatia au kufikiri kuhusu kitu fulani. "kitu fulani ambacho Yahwe Mungu hufikiri ni kiovu"

huvujika kwa agano lake

"kutotii agano lake"

yeyote ambaye ameshaenda

"kama unamkuta yoyote ambaye ameshaenda"

yeyote wa jeshi la mbinguni

"nyota yoyote"

hakuna kitu nilichokuamuru

"ambayo sijamwamuru yoyote kufanya"

ikiwa umeambiwa juu ya hili

Hii inaweza kusemwa kwa mfumo tendaji. "kama mtu anakuambia kuhusu hili tendo la kutotii"

fanya uchunguzi wa makini

Jina dhahania "uchunguzi" inaweza kusemwa kama kitenzi. "unapaswa kwa uangalifu uchunguzi kilichotokea"

Hitilafu hiyo imefanywa nchini Israeli.

Hii inaweza kusemwa kwa mfumo kazi.

Deuteronomy 17:5

Kwa kinywa cya mashahidi wawili, au watatu, yeye atakayekufa atauawa

Hapa "kinywa" uwakilisha ushuhuda wa mashahidi. Hii inaweza kutofasiriwa kwa mfumo kazi.

lakini kwa kinywa cha shahidi moja peke hapaswi kuawa

Hapa "kinywa" uwakilisha ushuhuda wa shahidi. Hii inaweza kutofasiriwa kwa mfumo kazi. "kama mtu mmoja peke anazungumza dhidi yake, basi unapaswa kumuawa"

Mkono wa shahidi unapaswa kuwa wa kwanza kumuawa, na baada ya hapo mkono wa watu wote

Hapa "mkono" uwakilisha mtu mzima. "Mashahidi wenyewe wanapaswa kuwa wa kwanza kumponda mawe. Basi watu wote watamuawa kwa mponda mawe"

na utaondoa uovu kutoka miongonu mwenu

Jina kuvumshi "uovu" inaweza kusemwa kama kuvumishi. "unapaswa kumuondoa miongoni mwa Waisraeli mtu huyu ambaye afanya uovu huu" au unapaswa kumuawa mtu huyu muovu"

Deuteronomy 17:8

Habari ya jumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

ikiwa jambo linatokea

"kama kuna jambo" au "kama kuna hali"

haki ya mtu mmoja na mwingine

"haki" ni mamlaka ya kisheria kufanya kitu fulani au kumiliki kitu fulani.

ndani ya malango ya mji wako

Hapa "malango ya mji" uwakilisha miji. "ndani ya miji yenu"

utatafuta ushauri wako

Jina "ushauri" inaweza kusemwa kama kitenzi. "utawauliza wakushauri"

watakupa uamuzi

Jina "uamuzi" inaweza kusemwa kama kitenzi. "watafanya maaumuzi juu ya mambo"

Deuteronomy 17:10

Unapaswa kufuata sheria uliyokupa

Mtu kutii kile makuhani na mwamuzi wanachoamua husemwa kama mtu kimwili anafuata kwa nyuma sheria. Hii inaweza kusemwa kwa mfumo kazi. "Unapaswa kutii kile mwamuzi na makuhani wanamua kuhusu jambo"

Usigeuke kwa kile wanachokuambia, kwa mkono wa kulia au kushoto.

Mtu asipofanya hasa kila mwamuzi na makuhani wanasema anasemwa kama alikuwa ameiacha njia sahihi/

Deuteronomy 17:12

kwa kutomsikiliza kuhani...wala kwa kutomsikiliza mwamuzi

"na hakuna kumtii kuhani...wala hakuna kumtii mwamuzi"

utaondoa mbali uovu toka Israeli.

Jina kivumushi "uovu" inaweza kutofasiriwa kama kivumushi. "unapaswa kumwondoa mtu toka miongoni mwa Waisraeli mtu afanyae kitu kiovu" au "unapaswa kumuawa mtu huyu muovu"

Watu wote wanapaswa kusikiliza na kuogopa, na kutotenda kwa kiburi tena

Inamaanisha kwamba wakati watu wanasikia kuhusu mtu aliyeuawa kwa kufanya kwa kiburi, wataogopa na hawatafanya kwa kiburi wenyewe.

Deuteronomy 17:14

Habari ya jumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Wakati ulipokuja kwenye nchi

Neno "kuja kwenye" linaweza kutofasiriwa kama "kwenda kwa" au "kuingia."

basi unasema, 'Nitaweka mfalme juu yangu, kama mataifa yote ambayo yananizunguka'

Hii ina nukuu ndani ya nukuu. Nukuu ya moja kwa moja inaweza kusemwa kama nukuu isiyo ya moja kwa moja. "basi unaweza kuamua kwamba unahitaji mfalme kama wa watu wa mataifa ambayo yana wafalme"

weka mfalme juu yangu

Kumpa mtu mamlaka kutawala kama mfalme huko Israeli husemwa kama watu walikuwa wanamweka mtu katika sehemu iliyo juu yao.

kama matiafa yote ambayo yananizunguka mimi

"kama mataifa yaliozunguka"

mataifa yote

mataifa yote Hapa "matiafa" uwakilisha mtu anaishi kwenye mataifa.

moja kutoka miongoni mwa ndugu zenu

"moja ya Waisraeli wenzako"

mgeni, ambaye siyo ndugu yako

Yote haya makundi ya maneno umaanisha kitu kile. Ote urejea kwa mtu ambaye siyo Mwiisraeli.

Deuteronomy 17:16

kwa kuwa Yahwe alikwisha sema kwako, "Haupaswi kuanzia sasa kamwe usirudi njia hiyo tena'

Hii imekuwa nukuu ndani ya nukuu. Nukuu ya moja kwa moja inaweza kusemwa kama nukuu isiyo ya moja kwa moja. "kwa kuwa Yahwe amekwisha sema kwamba haupaswi kamwe kurudi Misri tena"

ili moyo wake usiondoke kutoka kwa Yahwe

Hapa "moyo" urejea kwa mtu mzima. Wafalme mara nyingi walioa wanawake kutoka mataifa mengine ambayo yaliabudi miungu tofauti. Mfalme wa Israeli ambaye anaanza kuabudu miungu ya uongo wa mke wake husemwa kama moyo wake umegeuka mbali kutoka Yahwe.

Deuteronomy 17:18

Wakati akaapo kwenye kiti cha enzi chake cha ufalme

Hapa "kiti cha enzi" uwakilisha ngu ya mtu na mamlaka kama mfalme. Kukaa kwneye kiti cha enzi umaanisha kuwa mfalem.

kutoka sheria ambayo ilikuwa mbele ya makuhani, ambao ni Walawi

"kutoka kwenye nakala ya sheria ambayo makuhani wa kilawi walitunza"

ili kuyashika yote maneno ya sheria na amri hizi, kuzitama

Haya makundi ya maneno umaanisha kimsingi kitu kilekile na kusisitiza kwamba mfalme anapaswa kutii sheria zote za Mungu.

Deuteronomy 17:20

ili kwamba moyo wako haujainuliwa zaid ya ndugu zake

Hapa "moyo wake" ujrea kwa mtu mzima. Mfalme kuwa na kiburi inasemwa kama moyo uliinuliwa

ili kwamba asiache njia kutoka kwa amri, kwa mkono wa kulia na wa kushoto.

Mfalem kutotii amri za Mungu husemwa kama mtu anaiacha njia sahihi.

kuongoze maisha yake

Siku ndefu ni mfano wa maisha marefu. Hii inaweza kutofasiriwa sawasawa na "kuzidisha siku yako" katika 4"25

Deuteronomy 18

Deuteronomy 18:1

Habari ya jumla

Musa aendelea kuwambia watu kile Yahwe anahitaji wao wafanye.

hatutakuwa na sehemu wala urithi pamoja na Israeli.

Walawi hawapokei ardhi yoyote kutoka kwa Yahwe husemwa kama hawatapokea urithi.

hakuna sehemu

"hakuna sehemu" au "hakuna sehemu"

miongoni mwa ndugu zake

"miongoni mwa makabila mengine ya Israeli" au miongoni mwa Waisraeli"

Yahwe ni urithi wao

Musa azungumza kwa heshima kwa Aroni na wazao wake watakuwa kwa kumtumikia Yahwe kama makuhani kama Yahwe alikuwa kitu watakachorithi.

Deuteronomy 18:3

yu kuhani

"madai ya makuhani" au "kushiriki kwa makuhani"

sehemu za ndani zaidi

Hii ni tumbo na matumbo.

unapaswa kumpa

"unapaswa kutoa kwa kuhani"

amemchagua yeye

Hapa "yeye" uwakilisha Walawi wote

kusimama kwa kutumika kwa jina la Yahwe

Hapa "jina la Yahwe" usimama kwa Yahwe mwenyewe na mamlaka yake. "kuwa watumishi wake maalumu" au " kutumika kama wawakilishi wa Yahwe"

yeye na watoto wake milele

Hapa "yeye" uwakilisha Walawi wote.

Deuteronomy 18:6

kutamani kwa roho yake yote

Hii ni nahau. "anatamani sani" au "anataka kweli"

basi anapaswa kutumika kwa jina la Yahwe Mungu wake

Hapa "jina" uwakilisha Yahwe na mamlaka yake. "kisha anapaswa kumtumikia Yahwe na Mungu wake kama kuhani"

anasimama huko mbele ya Yahwe

"ambaye anatumika kwenye mahali patakatifu kwa uwepo wa Yahwe"

urithi wa familia yake

Hiki ndicho kuhani angeweza kurithi kutoka kwa baba yake

Deuteronomy 18:9

Wakati unapokuja

Hapa "kuja" kunaweza kutofasiriwa kama "kwenda" au "kuingia"

haupaswi kujifunza kuchunguza machukizo ya mataifa hayo

Mungu achukia shughuli za kidini za watu kwa mataifa yanayowazunguka. Anawazingatia kuwa mbaya sana. Hapa "mataifa" uwakilisha watu.

haipaswi kupatikana kati yenu yeyote

Hii inaweza kusemwa kwa mfumo kazi. "Pasiwepo miongoni mwenu"

kumweka kijana wake au binti wake kwenye moto

"kutoa dhabihu watoto wake kwenye moto juu ya madhabahu"

yoyote atumiae uchawi ...aongea na roho

Hawa ni watu tofauti wanaotumia uchawi. Mungu amekataza kila aina ya uchawi. Kama hauna neno kwa aina hii ya watu, inaweza kusemwa kwa ujumla. "yeyote atumiae uchawi kujaribu kungundua nini kitatokea badae, kuelezea, au kuongea na roho wafu"

kufungua

kutumia uchawi kutabili baadaye

Deuteronomy 18:12

kuwaondoa

Hapa "wao" urejea kwa watu tayari wanaishi huko Kanani.

Kwa mataifa haya

Hapa "mataifa" usimama kwa ajili ya makundi ya watu ambao wanaishi Kanani.

kuwaondoa

"kuwaondoa" au kuwatoa nje"

Deuteronomy 18:15

Habari ya jumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Yahwe Mungu wenu atainua kwa ajili yenu nabii

Yahwe kuteua mtu kuwa nabii husemwa kama Yahwe uinua mtu juu.

moja ya ndugu zenu

"moja ya ndugu Waisraeli"

Hiki ndicho ulichouliza

Hapa "wewe" urejea kwa Waisraeli huko kwenye Mlima Horebu kuhusu miaka 40 ya awali.

huko Horebu siku ile ya kusanyiko

"siku ile mlipokusanyika pamoja huko Horebu"

siku ya kusanyiko, kusema, "Hebu tuache kusikia tena sauti ya Yahwe Mungu wetu, wala kuona moto wake mkuu tena, au tutakufa'

Hii ina nukuu ndani ya nukuu. Nukuu ya moja kwa moja inaweza kusemwa kama nukuu isiyo ya moja kwa moja. "siku ya kusanyiko wakati uliposema kwamba haukutaka kusikia sauti ya Yahwe Mungu wetu, wala kuona moto mkuu tena, kwa sababu uliogopa kwamba utakufa"

Hebu tuache kusikia tena sauti ya Yahwe Mungu wetu

Hapa "sauti" uwakilisha Yahwe anazungumza. "Hebu tuache kumsikia Yahwe Mungu wetu anazungumza tena"

Deuteronomy 18:17

Nitaunua nabii kwa ajili yenu

Yahwe kuteua mtu kuwa nabii husemwa kama Yahwe angeinua mtu juu.

kutoka miongoni mwa ndugu zenu

"kutoka miongoni wenzenu Waisraeli"

Nitaweka maneno yangu kwenye kinywa chake

Yahwe kumwambia nabii nini cha kusema husemwa kama Yahwe angeweka maneno kwenye kinywa cha nabii.

zungumza nao

"zungumza na watu wa Israeli"

usisikilize maneno yangu ambayo anazungumza kwa jina langu

Hapa "maneno" uwakilisha nini Yahwe asema. Hapa maneno "jina langu" uwakilisha Yahwe na mamlaka yake. "usimsikilize wakati azungumzapo ujumbe wangu"

kuhitaji hivyo

"Mimi nitamshikilia kuwajibika" au "Nitamwadhibu." Hapa "yeye" urejea kwa mtu asiyemsikiliza nabii.

Deuteronomy 18:20

Habari ya jumla

Yahwe aendelea kuzungumza

ambaye aongea neno kwa kiburi

Hapa "neno" uwakilisha ujumbe.

kwa jina langu

Hapa "jina langu" urejea kwa Yahwe mwenye na mamlaka yake.

neno ambalo sijakuamuru

Hapa "neno" uwakilisha ujumbe "ujumbe ambao sijakuamuru"

ambaye azungumza kwa jina la miungu mingine

Hapa "jina" uwakilisha miungu yenyewe au mamlaka yao. Hii inamaanisha nabii adai kwamba miungu ya uongo alimwambia kuzungumza ujumbe fulani.

Hivi ndivyo unapaswa kusema kwenye moyo wako

Hapa "moyo" uwakilisha mawazo ya mtu. "Unazungumza mwenywe" au "Unapaswa kusema mwenywe"

Tutagundua je ujumbe wa Yahwe ambao hajazungumza?

"Namna gani tunaweza kujua kama ujumbe ambao nabii amezungumza umetoka kwa Yahwe? Hapa "tu" urejea kwa watu wa Israeli.

Deuteronomy 18:22

Habari ya jumla

Yahwe aendelea kuzungumza

nabii azungumza kwa jina la Yahwe

Hapa "jina la Yahwe" urejea kwa Yahwe mwenyewe na mamlaka yake. "nabii adai kuzungumza nami" au "nabii adai kuzungumza na mamlka yangu"

nabii amezungumza kwa kiburi

"nabii amezungumza ujumbe huu pasipo mamlaka yangu"

Deuteronomy 19

Deuteronomy 19:1

Habari ya jumla

Musa bado anazungumza na watu wa Israeli.

Wakati Yahwe Mungu wenu huyapunguza mataifa

Yahwe kuwaharibu watu wanaoishi Kanani husemwa kama wamepungunzwa, kama mmoja angewapungunza kwa vipande vya nguo au kupungunza tawi la mti

mataifa

Hii uwakilisha makundi ya watu ambayo huishi huko Kanani.

wale ambao nchi Yahwe Mungu wenu anawapa

"yale mataifa ambayo yalikuwa yanaishi katika nchi ambayo Yahwe Mungu wenu anawapa"

kuja baada yao

"chukua nchi kutoka mataifa yale" au "miliki nchi baada ya yale mataifa yaliyoenda"

chagua miji mitatu

"chagua miji 3"

Unapaswa kujenga barabara

Walikuwa wanajenga barabara ili kwamba iwe rahisi kwa watu kusafiri kwa miji hii.

gawa mipaka ya ardhi yako kwa sehemu tatu

Ina maanisha kwamba moja ya miji waliochagua unapaswa kuwa kila sehemu ya nchi.

nchi ambayo Yahwe Mungu wenu anasababisha ninyi kurithi

Yahwe atoa nchi kwa watu wa Israeli husemwa kama watu walikuwa wanarithi nchi.

Deuteronomy 19:4

Hii sheria mpya

"Haya ni maelekezo" au "Huu ni mwelekeo"

kwa yeyote anayemuuwa mwingine

Neno "mtu" linaeleweka. "kwa mtu ambaye anamuuwa mtu mwingine"

na ambaye anakimbilia huko

"na ambaye hutorokea kwa moja ya miji hii" au "na ambaye akimbilia kwa moja ya miji hii"

kuishi

"kuokoa maisha yake." Maana kamili ya maelezo haya inaweza kufanywa wazi. "ili familia ya mtu aliyekufa hamuuwi kwa kulipiza kisasi"

yeyote anayemwua jirani yake hajui

Hapa "jiran" umaanisha mtu kwa jumla. "mtu yeyote ambaye anamwua mtu mwingine kwa ajali"

na hakumchukia hapo awali

"lakini hakumchukia jirani yako kabla hajamuuwa." Hii inamaanisha hapakuwa na kisababishio cha yeye kumuuwa jirani yake kwa makusudi.

kama wakati mtu huenda kwenye msitu...kukata kuni

Mwandishi hutoa hali ya kufikiri ambapo mtu amuuwa mtu mwingine kwa ajali.

kichwa kinapiga kutoka shimoni

sehemu ya chuma ya shoka hutoka kwenye kushughulikia.

kumpiga jirani yake ili afe

Hii inamaanisha kichwa cha shoka hugonga na kumuuwa jirani.

kwa moja ya miji hii na kuishi

"kwa moja ya miji hii kuokoa maisha yake." Inamaanisha kwamba familia ya mtu aliyekufa yaweza kulipisa kisasi. Mtu aliyemuuwa anayeweza kukimbilia kwa moja ya miji hii, na watu wa huko watamlinda.

Deuteronomy 19:6

Habari ya jumla

Musa bado anazungumza na watu wa Israeli.

mlipuko wa damu

Hapa "damu" uwakilisha mtu ambaye aliyeuwawa. "mlipuko wa damu" ni ndugu wa karibu wa mtu aliyeuwawa. Huyu ndugu anawajibika kwa kumwadhibu muuaji.

mmoja aliyechukua maisha

Hii ni nahau. "yule aliyemwua mtu mwingine"

kwa hasira kali

mtu aliye na hasira sana anazungumzwa kama hasira ni kitu kinachoweza kuwa moto.

Na anampiga

"Na mlipuko wa damu huwapiga mtu aliyemwua mtu mwingine"

ingawa mtu huyo hakuwastahili kufa, na hivyo hastahili adhabu ya kifo tangu hakumchukia jirani yake kabla ya hili kutokea

"ingawa mtu huyo hakuwastahili kufa tangu alimuuwa kwa ajali mtu mwingine na hakuwa adui wake"

Deuteronomy 19:8

Habari ya jumla

Musa bado anazungumza kwa watu wa Israeli

kukuza mipaka yako

"ukupa ardhi zaidi kumiliki"

kama alivyowaapia baba zako kufanya

"kama alivyowaahidi babu zenu kwamba atafanya"

kama utayashika hizi amri kuzifanya

"kama unatii amri zote hizi"

daima kutembea kaitka njia zake

Namna Mungu anahitaji mtu aishi au kutenda husemwa kama ilikuwa njia ya Yahwe au barabara. Mtu ambaye anamtii Yahwe husemwa kama alikuwa anatembea kwenye njia ya Yahwe au barabara.

kisha unapaswa kuongeza miji mitatu au zaidi kwa ajili yako

Maana kamili ya maelezo haya inaweza kufanywa wazi. "kisha unapaswa kuchagua miji mitatu zaidi kwa ajili ya mtu kutoroka kama amemuuwa mtu kwa ajili"

badala ya hii mitatu

"kwa nyongeza ya miji mitatu uliyoanzisha tayari"

Fanya hivi ili damu ya asiye na hatia isimwangwe.

Hii inaweza kusemwa kwa mfumo wa kazi. "Fanya hivi ili kwamba ndugu wa familia wasiuwe mtu asiye na hatia"

katikati mwa nchi

"kwenye ardhi" au "kwenye wilaya"

Yahwe Mungu wenu anawapa kama urithi

Nchi ambayo Yahwe anawapa watu wa Israeli husemwa kama ilikuwa urithi.

ili usiwe na hatia ya damu kwako

Watu wa Israeli kuwa na hatia kwa ajili ya mtu kufa kwa sababu hawakujenga mji ambao angekuwa salama kutoka kwa "mlipizi wa damu" inasemwa kama hatia ya kifo chake kiko juu yao.

damu ya hatia

Hapa "damu" uwakilisha uhai na "hatia ya damu" urejea kwa hatia ya mtu aliyo nayo kwa kuuwa mtu asiye na hati.

labda iwe juu yenu

Hii ina maana ya kwamba ndugu wa familia anauwa mtu asiye na hati, basi watu wote wa Israeli watakuwa na hatia kwa kuruhusu hilo kufanyika.

Deuteronomy 19:11

jirani yake

Hapa "jirani" umaanisha mtu yeyote kwa jumla.

amelala kumngojea yeye

Maana kamili ya maelezo haya yanaweza kufanywa wazi. "jifiche na kusubiri kwa kusudi la kumuuwa" au " kupanga kumuwa yeye"

kuinuka dhidi yake

Hii ni nahau. "kumvamia yeye"

na kujeruhiwa na kufa

"na kuumiza yeye ili kwamba afe" au "na kumuuwa yeye"

unapaswa kutuma na kumleta nyuma kutoka huko

"unapaswa kutuma mtu kumchukua yeye na kumleta nyuma kutoka kwenye mji ambao alotorokea"

kumgeuza

Hii ni nahau "kumtoa yeye"

kwenye mkono wa ndugu wahusika

Hapa "mkono" uwakilisha mamlaka ya mtu.

anaweza kufa

"muuaji anaweza kufa" au " ndugu ahusikiae anaweza kumuuwa muuaji"

Macho yako hayapaswi kumuonea huruma

Hapa "macho yako" uwakilisha mtu mzima.

unapaswa kuondosha kutoka Israeli

Hapa "hatia ya damu" uwakilisha hatia kwa muuajia mtu asiye na hatia.

kutoka Israeli

Hapa "Israeli" urehea kwa watu wa Israeli.

Deuteronomy 19:14

Habari ya jumla

Musa bado anazungumza na watu wa Israeli.

Haupaswi kuondoa alama ya ardhi kwa jirani yako

Maana kamili ya maelezo haya inaweza kufanywa wazi. "Haupaswi kuchukua ardhi kutoka kwa jirani yako kwa kuondoa alama kwenye mipaka ya ardhi yake"

wao kuweka mahali

"ambayo babu zenu waliweka"

muda mrefu uliopita

Musa anamaanisha kwamba wakati watu walipoishi kwenye nchi kwa muda mrefu, hawapaswi kuondoa mipaka ambayo babu zao walifanya wakati walipochukua nchi.

katika urithi wenu ambayo mtarithi, katika nchi ambayo Yahwe Mungu wenu anawapa kumiliki

Yahwe kuwapa nchi kwa watu wa Israeli husemwa kama walikuwa wanarithi nchi.

Deuteronomy 19:15

Habari ya jumla

Musa bado anazungumza na watu wa Israeli.

Shahidi mmoja pekee

"Shahidi mmoja" au "shahidi mmoja pekee"

hapaswi kuinuka dhidi ya mtu

Hapa "kuinuka" umaanisha kusimama mahakamani na kusema kinyume ya mtu kwa jaji. "haupaswi kusema kwa majaji kuhusu kibaya alichofanya mtu"

katika jambo lolote ambalo amefanya dhambi

"wakati wowote ambao mtu ufanya kitu kibaya"

kwa kinywa cha mashahidi wawili, au kwa kinywa cha mashahidi watatu

Hapa "kinywa" uwakilisha nini mashahidi wanasema. Inamaanisha kwamba kunapaswa angalau kuwa na mashahidi wawili au watatu.

lazima jambo lolote lihakikishwe

Hii inaweza kusemwa kwa mfumo kazi. "utahakikisha kwamba mtu ana hatia"

Kama hivyo

"Wakati" au "kama"

shahidi asiye wa haki

"shahidi ambaye anatarajia kumdhuru mtu mwingine"

kuinuka kinyume cha mtu yoyote kushuhudia kinyume cha uovu wake.

Hapa "kuinuka" umaanisha kusimama mahakamani na kusema kinyume cha mtu kwa jaji. "umwambia jaji kwamba mtu alifanya dhambi ili kumuingiza mtu kwenye shida" au "umwambia jaji kwamba mtu alifanya dhambi, ili kwamba jaji amhukumu"

Deuteronomy 19:17

Habari ya jumla

Musa aendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

mmoja kati ya yule utata upo

"mmoja kati hakubaliani na mwingine"

anapaswa kusimama mbele ya Yahwe, mbele ya makuhani na waamuzi

Hii inamaanisha watu wawili wanapaswa kwenda mahali patakatifu ambapo uwepo wa Yahwe ukaa. Mahali patakatifu wako makuhani na waamuzi ambao wana mamlaka kufanya maaumizi ya kisheria kwa Yahwe.

kusimama mbele ya Yahwe, mbele ya makuhani na waamuzi

Maneno "kusimama mbele" ni nahau. Inamaanisha kwenda kwa mtu aliye na mamlaka na kumwacha afanye maamuzi ya kisheria kuhusu jambo.

Waamuzi wanapaswa kuchunguza kwa uangalifu

"Waamuzi wanapaswa kufanya kazi kwa nguvu sana kuamua kilichotokea"

basi lazima umfanyie, kama alivyotaka kumfanyia ndugu yake

"basi unapaswa kumwadhibu shahidi muongo vilevile kama alivyokutaka wewe umwazibu mtu mwingine"

utaondoa uovu kutoka miongoni mwenu

Hili jina"uovu" linaweza kusemwa kama kivumishi. "kwa kumwadhibu shahidi muongo, utaacha uovu huu ndani ya taifa lenu"

Deuteronomy 19:20

Basi wale wanaobaki

"Wakati unapomwadhibu shahidi muongo, watu wengine "

watasikia na kuogopa

Maana kamili ya maelezo haya inaweza kufanywa wazi. "watasikia kuhusu adhabu na kuogopa kupata adhabu"

hawatafanya tena aina ya uovu

"kamwe tena hawatafanya uovu kama huo"

Macho yako hayapaswi kuona huruma

Hapa "macho" urejea kwa mtu mzima. "Haupaswi kumuonea huruma" au "Haupaswi kumuonyesha huruma"

maisha yatalipa kwa maisha... mguu kwa mguu.

Hapa maneno yamefupishwa kwa sababu maana inaeleweka. Inamaanisha watu wanapaswa kumwadhibu mtu kwa njia ileile alivyo mfanyia mwingine.

Deuteronomy 20

Deuteronomy 20:1

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Pindi utokapo kwenda vitani kupigana dhidi ya adui zako

"Utakapokwenda kupigana katika vita dhidi ya adui zako"

na kuona farasi, vibandawazi

Watu walichukulia jeshi lenye farasi wengi na vibandawazi kuwa na nguvu sana. Maana kamili ya kauli hii yaweza kuwekwa wazi.

yeye aliyekuleta juu kutoka nchi ya Misri.

Yahwe aliwaleta watu kutoka Misri hadi Kaanani. Ilikuwa kawaida kutumia neno la "juu" kuzungumzia safari ya kutoka Misri kwenda Kaanani. "Yahwe aliyekuongoza kutoka katika nchi ya Misri"

Deuteronomy 20:2

Taarifa ya Jumla:

Musa aliendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

kuongea na watu

"zungumza na maaskari wa Israeli"

Msidhofishe moyo wenu. Msiohofu au kutetemeka. Msiwaogope

Misemo hii minne yote ina maana moja na inasisitiza kwa nguvu ya kwamba hawapaswi kuogopa. Iwapo lugha yako haina njia nne ya kuelezea wazo hili, unaweza kutumia chini ya njia nne.

Msidhofishe moyo wenu

Hapa "moyo" inawakilisha ujasiri wa watu. Kwa moyo kudhoofika ni lugha nyingine inayomaanisha "Usiogope"

Yahwe Mungu wenu ndiye aendae pamoja nanyi kupigana kwa ajili yenu dhidi ya maadui zenu

Yahwe kuwashinda adui wa watu wa Israeli inazungumziwa kana kwamba Yawhe alikuwa mpiganaji ambaye angepigana pamoja na watu wa Israeli.

kuwaokoa

"kukupa ushindi"

Deuteronomy 20:5

Taarifa ya Jumla:

Musa anasema kile ambacho maakida wa jeshi wanapaswa kuzungumza kwa watu wa Israeli kabla ya vita.

Maakida wanapaswa kuzungumza

Moja ya kazi za maakida ilikuwa kuamua nani ataondoka jeshini. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi.

Ni mtu yupi ... Acha aende na arudi nyumbani kwake

"Iwapo askari yeyote hapa amejenga nyumba mpya na hajaiweka wakfu, anapaswa kurudi katika nyumba yake"

ili kwamba asife vitani na mtu mwingine aiweke wakfu

Maafisa wanaelezea tukio ambalo lingeweza kutokea kwa askari. "ili kwamba, kama atakufa vitani, mtu mwingine hataweka wakfu nyumba yake badala yake"

Deuteronomy 20:6

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuelezea matukio yanayomruhusu mtu kuondoka jeshini.

Kuna yeyote ambaye amepanda ... Acha aende nyumbani

"Iwapo askari yeyote hapa ana shamba la mzabibu, lakini bado hajavuna matunda yake, anapaswa kurudi nyumbani kwake"

ili kwamba asife vitani na mtu mwingine afurahie matunda yake

Afisa anaelezea tukio ambalo linaweza kutokea kwa askari. "ili kwamba, kama atakufa vitani, mwanamume mwingine asivune matunda yake badala yake"

Ni mtu yupi aliyeposa kuoa mwanamke ... Acha aende nyumbani

"Iwapo askari yeyote hapa ameahidi kumuoa mwanamke, lakini bado hajamuoa, anapaswa kurudi nyumbani kwake"

ili kwamba asife vitani na mume mwingine amuoa

Afisa anaelezea tukio ambalo linaweza kutokea kwa askari. "ili kwamba, kama atakufa vitani, mwanamume mwingine asimuoe mwanamke badala yake"

Deuteronomy 20:8

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuelezea matukio yanayomruhusu mtu kuondoka jeshini.

Ni mwanaume gani aliye hapa ambaye ni mwenye hofu au mnyonge? Acha aende na arudi nyumbani kwake

"Kama askari yeyote hapa ana hofu na sio jasiri, anapaswa kurudi nyumbani kwake"

hofu au mnyonge

Maneno haya yote mawili yana maana moja. "anaogopa kupigana vitani"

moyo wa ndugu yake usiyeyuke kama moyo wake mwenyewe

Hii ni lahaja. "Muisraeli mwingine hawi na hofu kama anaogopa"

moyo wa ndugu yake ... moyo wake mwenyewe

Hapa "moyo" unawakilisha ujasiri wa mtu.

wanapaswa kuteua majemedari juu yao

"maafisa wanapaswa kuteua watu kuwa majemedari na kuwaongoza watu wa Israeli"

Deuteronomy 20:10

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Wakati mtokapo kushambulia mji

Hapa "mji" unawakilisha watu. "Utakapokwenda kushambulia watu wa mji"

wafanye watu hao toleo la amani

"wape watu wa mji fursa ya kujisalimisha"

kufungua malango yao kwako

Hapa "malango" yana maana ya malango ya mji. Msemo wa "kufungua malango yao kwako" inawakilisha watu kujisalimisha na kuruhusu Waisraeli kuingia katika mji. "kuruhusu kuingia mji wao kwa amani"

watu wote wanaopatikana ndani yake

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "watu wote katika mji"

wanapaswa kulazimishwa kukufanyia kazi na wanapaswa kukutumikia.

"wanapaswa kuwa watumwa wako"

Deuteronomy 20:12

Lakini kama haitengenezi amani kwenu

Hapa "haitengenezi" ina maana ya mji ambao unawakilisha watu. "Lakini kama watu wa mji hawatajisalimisha" au "Lakini kama watu wa mji hawatapokewa ahadi ya amani"

Deuteronomy 20:14

wadogo

"watoto"

na nyara zake zote

"na vitu vyote vya thamani"

mateka

Hivi ni vitu vya thamani ambavyo watu wanaoshinda vita huchukua kutoka kwa watu waliowashambulia.

miji yote

Hapa "miji" inawakilisha watu. "watu wote wanaoishi katika miji"

Deuteronomy 20:16

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Katika miji ya watu hawa ambayo Yahwe Mungu wenu anawapa kama urithi

Miji ya Kaanani ambayo Yahwe anawapa watu inazungumziwa kana kwamba miji ilikuwa urithi wa watu.

mnapaswa kutunza chochote kilicho na uhai

"hampaswi kuacha kiumbe chochote hai". Hii inaweza kuwekwa katika hali ya chanya. "Mnapaswa kuua kila kiumbe hai"

mnapaswa kabisa kuwaangamiza

"mnapaswa kuwaangamiza kabisa makundi haya ya watu"

Fanya hivi ili kwamba

"Yaangamize mataifa haya ili kwamba"

kufanya katika njia za machukizo ... miungu yao

"kufanya katika njia za machukizo kama watu wa mataifa walivyofanya kwa miungu yao"

Kama mtafanya, mtafanya dhambi dhidi ya Yahwe Mungu wenu

"Kama mtafanya kama watu hawa, mtafanya dhambi dhidi ya Yahwe Mungu wenu"

Deuteronomy 20:19

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

mkipigana

"kupigana vitani"

kwa kushika shoka dhidi yao

"kwa kukata chini miti kwa shoka"

Kwa maana mti wa kondeni mtu ambaye atauzingira?

Swali hili la balagha linawakumbusha watu kile ambacho walipaswa kukijua. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Kwa maana mti ya kondeni sio watu, kwa hiyo sio adui zako"

unaijua siyo miti ya chakula

"unajua sio miti ambayo huotesha matunda ya kula"

utajenga maburuji

Hivi ni vifaa na miundo, kama vile ngazi na minara, ambayo inahitajika kujenga maburuji kwa mji.

mpaka ianguke

Hii ni lahaja. "mpaka watu wa mji watakaposhindwa vita"

ianguke

Hapa "ianguke" ina maana ya mji ambao unawakilisha watu wa mji.

Deuteronomy 21

Deuteronomy 21:1

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Iwapo mtu amekutwa kauwawa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. Iwapo mtu amemkuta mtu ambaye mtu mwingine amemuua"

kalala shambani

Mtu aliyekufa amelala shambani.

haijulikani aliyemshambulia

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "na hakuna mtu anayejua aliyemshambulia"

wanapaswa kupima katika miji

"wanapaswa kupima urefu katika miji"

yule aliyeuawa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "yeye ambaye mtu amemuua" au "maiti"

Deuteronomy 21:3

hajawahi kubebeshwa nira

"hajawahi kuvaa nira"

litiririkalo maji

Hii ni lahaja ya maji yanayotiririka. "kijito"

bonde ambalo halijawahi kulimwa wala kupandwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "bonde ambalo hakuna mtu hajalima nchi wala kupandwa mbegu"

Deuteronomy 21:5

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

wanapaswa kuja mbele

"wanapaswa kuja bondeni"

kwa maana Yahwe Mungu wako amewachagua wamtumikie yeye

"kwa sababu makuhani ndio wao ambao Yahwe Mungu wako amewachagua kumtumikia"

Yahwe Mungu wako

Musa anazungumza na Waisraeli kana kwamba alikuwa akizungumza na mtu mmoja, kwa hiyo neno "wako" ni katika umoja.

kutoa baraka kwa watu

"kubariki watu wa Israeli"

katika jina la Yahwe

Hapa lugha nyingine "katika jina la" ina maana ya Yahwe na mamlaka yake. "kama yule asemavyo na kufanya kile Yahwe mwenyewe angesema na kufanya"

sikiliza ushauri wao

"sikiliza kile makuhani wanachosema"

kwa maana neno lao litakuwa hukumu

Hapa lugha nyingine "neno lao" ina maana ya kile makuhani wanachosema. "kwa sababu chochote makuhani wanchosema, huo utakuwa uamuzi wao"

katika kila mtafaruku na ugomvi

"kila wakati watu wanapokuwa mahakamani kwa sababu ya kutokuelewana baina yao au mtu kudhuru mtu mwingine"

Deuteronomy 21:6

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

mtamba aliyevunjwa shingo

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "mtamba ambaye shingo yake ilivunjwa na makuhani"

na wanapaswa kutoa suhulisho juu ya jambo hilo

"na wanapaswa kushuhudia kwa Yahwe juu ya jambo hili"

Mikono yetu haijamwaga damu hii

Hapa "mikono" ni lugha nyingine ya mtu mzima na "kumwaga damu" ni lugha nyingine ya kumuua mtu asiye na hatia. "Hatukumuua mtu huyu asiyekuwa na hatia"

wala macho yetu hayajaona suala hili

Hapa "macho" yana maana ya mtu mzima. "na hatuona mtu yeyote akimuua mtu huyu"

Deuteronomy 21:8

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuwaambia viongozi kile wanachopaswa kusema watakapoosha mikono yao juu ya mtamba. Anazungumza nao kana kwamba anazungumza na mtu mmoja, kwa hiyo maneno "wako" na "kwao" ni katika umoja.

ambao umewakomboa

Yahwe kuwaokoa watu wa Israeli kutoka utumwani Misri inazungumziwa kana kwamba Yahwe alilipa pesa kuwakomboa watu wake kutoka utumwani.

na usiweke hatia juu ya umwagaji damu usio na kosa miongoni mwa watu wako Israeli

Hii ni lahaja. "na usiwafanye watu wa Israeli kana kwamba wana hatia ya kuua mtu asiyekuwa na hatia"

Kisha umwagaji damu utasamehewa kwao

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Kisha Yahwe atasamehe watu wake Israeli kwa kifo cha mtu asiyekuwa na hatia"

utaweka mbali umwagaji damu usio na hatia miongoni mwenu

"hautakuwa na hatia tena kwa kuua mtu asiyekuwa na hatia"

yaliyo mema machoni pa Yahwe

Maneno "machoni pa Yahwe" ni lugha nyingine ya "kile Yahwe anachofikiri ni sahihi"

Deuteronomy 21:10

Taarifa ya Jumla

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba alikuwa akizungumza na mtu mmoja, kwa hiyo maneno "zako" na "yako" ni katika umoja.

Utakapokwenda

"nyie ambao ni askari nendeni nje"

nawe ukamtamani

"Unataka kulala naye"

kutaka kujitwalia awe mke wako

"unataka kumuoa"

atanyoa nywele zake

"atanyoa nywele kutoka katika kichwa chake"

kukata kucha zake

"kukata kucha zake"

Deuteronomy 21:13

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba alikuwa akizungumza na mtu mmoja, kwa hiyo maneno "zako" na "yako" ni katika umoja.

atazivua nguo alizokuwa amezivaa

Atafanya hivi baada ya mwanamume kumleta katika nyumba yake na atakaponyoa nywele na kukata kucha kama zilivyotajwa katika 21:10. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "atazivua nguo zake za watu wake na kuvaa nguo za Kiisraeli"

wakati alipochukuliwa mateka

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ulipomchukua mateka"

mwezi mzima

"mwezi mzima kamili" au "mwezi kamili"

Lakini usipofurahishwa naye

Unaweza kufanya hivi kuwa wazi ya kwamba mwanamume alilala na mwanamke. "Lakini ukilala naye na kisha kuamua ya kwamba haumtaki kama mkeo"

kumruhusu aondoke apendaye yeye

"mruhusu aondoke atakapo yeye"

kwa sababu umemdhalilisha

"kwa sababu umemuabisha kwa kulala naye na kisha kumfukuza"

Deuteronomy 21:15

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

a mmoja wao amempenda na mwingine kamchukia

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. Maana zaweza kuwa 1) "na mwanamume anampenda mmoja wa wake zake na kumchukia mke mwingine" au 2) "na mwanamume anampenda mke mmoja zaidi ya anavyompenda mke mwingine"

na wote wamekwisha mzalia watoto

"na wake wote wawili wakapata watoto kupitia kwake"

kama mzawa wa kwanza ni wa mke asiyependwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "kama mzawa wa kwanza ni wa mke ambaye mwanamume anamchukia"

basi katika siku ambayo mwanamume

"pale ambapo mwanamume"

mwanamume atakapowarithisha mali zake wanawe

"mwanamume akatoa mali yake kwa wanawe kama urithi"

hapaswi kumfanya mwana wa mke ampendaye kuwa mzawa wa kwanza kabla ya mwana wa mke amchukiaye

"hapaswi kumfanya mwana wa mke anayempenda kana kwamba alikuwa mwana wa kwanza badala ya mwana wa mke asiyempenda"

mara mbili ya sehemu

"mara mbili zaidi"

huyo mwana ni mwanzo wa nguvu zake

Hii ni lahaja. "mwana huyo ndiye anayeonyesha ya kwamba mwanamume huyo anaweza kuwa baba wa wanawe"

Deuteronomy 21:18

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

ambaye hatatii sauti ya baba yake au sauti ya mama yake

Hapa "sauti" ni lugha nyingine kwa kile mtu anachozungumza. "ambaye hatatii kile baba yake au mama yake anasema"

kurekebishwa

"wanamuadhibu kwa kutenda ubaya wake" au "wanamfundisha na kumuelekeza"

anapaswa kumshika na kumleta mbele

"wanapaswa kumlazimisha kutoka nje"

Deuteronomy 21:20

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja.

Huyu mwanetu

"Mwana wetu"

hataki kusikia sauti zetu

Hapa "sauti" ni lugha nyingine kwa kile mtu anasema au lugha nyingine ya mtu mzima. "hatafanya kile ambacho tunamwambia kufanya" au "hatatutii".

mwasherati

mtu ambaye hula na kunywa sana

mlevi

mtu ambaye hunywa sana kileo na kulewa mara kwa mara.

kumpiga kwa mawe hadi kufa

"kutupa mawe kwake mpaka afe"

mtaondoa uovu miongoni mwenu

Kivumishi "uovu" kinaweza kutafsiriwa kama msemo wa nomino. "unapaswa kuondoa miongoni mwa Waisraeli mtu ambaye anafanya uovu huu" au "mnapaswa kumuua mtu huyu muovu"

Israeli yote

Neno "Israeli" ni lugha nyingine la watu wa Israeli. "Watu wote wa Israeli"

tasikia juu ya hili na kuogopa

Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "atasikia juu ya kilichotokea kwa mwana na kuogopa ya kwamba watu watamuadhibu pia"

Deuteronomy 21:22

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba alikuwa akizungumza na mtu mmoja, kwa hiyo maneno "zako" na "yako" ni katika umoja.

Iwapo mwanamume kafanya dhambi inayostahili kifo

"Iwapo mwanamume amefanya jambo baya sana hadi unahitajika kumuadhibu kwa kumuua"

akauwawa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "kumuua" au "utamuua".

kwa kunyongwa juu ya mti

Maana zaweza kuwa 1) "na baada ya kufa unamnyonga ju ya mti" au 2) "na utamuua kwa kumyonga katika nguzo ya mbao"

unamzika siku hiyo

"mzike katika siku hiyo hiyo ambayo umemuua"

kwa maana yeyote anyongwaye amekwisha laaniwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. Maana zaweza kuwa 1) "kwa sababu Mungu hulaani kila mtu ambaye watu humyonga kwenye miti" na 2) "watu huwanyonga mtini wale ambao Mungu amewalaani"

usitie najisi nchi

kwa kukiacha kitu ambacho Mungu amekilaani kikining'inia juu ya mti.

Deuteronomy 22

Deuteronomy 22:1

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba alikuwa akizungumza na mtu mmoja, kwa hiyo maneno "zako" na "yako" ni katika umoja.

akikosea njia

"kutembea kutoka kwa mmiliki wake"

ukajificha kwao

Hii ni lahaja. "fanya kama vile hauwaoni" au "ondoka bila kutenda jambo lolote"

Iwapo Muisraeli mwenzako hayupo karibu nawe

"Kama Muisraeli mwenzako anaishi mbali na kwako"

au kama haumfahamu

"au kama haujui ni nani mmiliki wa mnyama ni nani"

na lazima uwe naye mpaka pale mwenyewe atakapomtafuta

"na unapaswa kukaa na mnyama mpaka pale mmiliki atakapokuja kumtafuta"

Deuteronomy 22:3

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo maneno "unapaswa" ni katika umoja

Unapaswa kufanya vivyo hivyo kwa punda wake

"Unapaswa kurudisha punda wake katika njia hiyo hiyo"

unapaswa kufanya vivyo hivyo na vazi lake

"Unapaswa kurudisha mavazi yake katika njia hiyo hiyo"

hautakiwi kujificha

Hii ni lahaja. "haupaswi kufanya kana kwamba hauoni ya kuwa amepoteza kitu" au "haupaswi kuondoka bila kufanya kitu"

hakika unapaswa kumsaidia kumwinua tena

"unapaswa kumsaidia Muisraeli mwenzako kumuinua mnyama asimame kwa miguu yake"

Deuteronomy 22:5

Taarifa ya Jumla:

Musa bado anazungumza na watu wa Israeli.

kinachokusudiwa kwa mwanamume

"nguo za wanaume"

Deuteronomy 22:6

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza na Waisraeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo maneno "yako" ni katika umoja.

kiota cha ndege

nyumba ambayo ndege hujitengenezea kwa kutumia vijiti, nyasi, mimea, na matope.

kikiwa na makinda ya ndege au mayai ndani mwake

"na watoto wa ndege aumayai ndani ya kiota"

na mama yao akiwa juu yao

"na mama wa ndege akikalia juu ya makinda ya ndege"

siku zako ziweze kurefushwa

Siku ndefu ni lugha nyingine kwa maisha marefu. "kuweza kuishi muda mrefu".

Deuteronomy 22:8

Taarifaya Jumla:

Musa anazungumza na Waisraeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo maneno "yako" hapa ni katika umoja.

kitalu kwa ajili ya paa yako

uzio ulio chini ukizunguka ukingo wa paa ili watu wasianguke kutoka kwenye paa.

ili usilete damu juu ya nyumba yako

Damu ni alama ya kifo. "ili kwamba isiwe kosa ya nyumba yako iwapo mtu atakufa"

mtu akianguka kutoka pale

"kama mtu yeyote ataanguka kutoka kwenye paa kwa sababu haiukuweka kitalu"

Deuteronomy 22:9

Taarifaya Jumla:

Musa anazungumza na Waisraeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo maneno "yako" hapa ni katika umoja.

ili kwamba mavuno yote yasichukuliwe na sehemu takatifu

Maneno "sehemu takatifu" ni lugha nyingine ya makuhani wanaofanya kazi katika sehemu takatifu. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ili kwamba makuhani katika sehemu takatifu ya Yahwe wasichukue mavuno yote" au "ili kwamba usitie najisi mavuno yote na makuhani wasikuruhusu kuyatumia".

na matunda ya mzabibu

"na matunda ambayo huota katika shamba la mzabibu"

sufu

manyoya malaini, yalikunjika ambayo huota kwa kondoo

kitani

uzi unaotengezwa kutokana na mmea wa kitani

Deuteronomy 22:12

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza na Waisraeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo maneno "yako" hapa ni katika umoja.

pembe

"manyamunyamu". Hizi ni nyuzi ambazo zimefungwa pamoja na kuning'inizwa kutoka kwenye pembe moja ya joho.

za nguo

Nguo ndefu ambalo mtu huvaa juu ya mavazi yake mengine.

Deuteronomy 22:13

Taarifaya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

na kisha kumtuhumu kwa vitu vya aibu

"na kisha kumtuhumu yeye kulala na mtu mwingine kabla hajaolewa"

na kumharibia sifa yake

Nomino inayojitegemea ya "sifa" inaweza kutafsiriwa kama msemo wa kitenzi. "na kufanya watu wengine kufikiri kuwa yeye ni mtu mbaya"

lakini nilipomkaribia

Hii ni njia ya upole ya kusema "kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mtu". "lakini nilipolala naye"

sikukuta ushahidi wa ubikira kwake

Nomino inayojitegemea ya "ushahidi" inaweza kutafsiriwa kama msemo wa kitenzi. "hakuweza kutoa ushahidi kwangu ya kwamba alikuwa bikira"

Deuteronomy 22:15

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

wanatakiwa kupeleka ushahidi wa ubikira wake

Nomino inayojitegemea ya "ushahidi" inaweza kutafsiriwa kama msemo wa kitenzi. "anapaswa kupeleka kitu ambacho kitakuwa ushahidi ya kwamba alikuwa bikira"

Deuteronomy 22:16

Taarifa ya Jumla:

Musa bado anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

amemtuhumu na vitu vya aibu

Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "amemtuhumu kwa kulala na mtu mwingine kabla hajamuoa"

Sikukuta ushahidi wa ubikira kwa binti yako

Nomino zinazojitegemea za "ushahidi" na "bikira" zinaweza kutafsiriwa kama misemo ya vitenzi. "Binti yenu hakuweza kuthibitisha ya kuwa alikuwa bikira"

Lakini ushahidi huu hapa wa ubikira wa binti yangu

Nomino zinazojitegemea za "ushahidi" na "bikra" vinaweza kutafsiriwa kama misemo ya vitenzi. "Lakini hii inathibitisha ya kuwa binti yangu alikuwa bikira"

Kisha watatandaza shuka mbele ya wazee wa mji

Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "Na kisha mama na baba watatoa nguo yenye doa la damu kwa wazee kama ushahidi ya kuwa alikuwa bikira"

Deuteronomy 22:18

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

nao wanapaswa kumtoza faini

"na wanapaswa kumfanya alipe kama adhabu"

shekeli mia moja

"Shekeli 100"

na kumpatia baba wa binti

"na kumpa pesa kwa baba wa binti"

kasababisha sifa mbaya kwa bikra wa Israeli

Nomino inayojitegemea "sifa" inaweza kutafsiriwa kama msemo wa kitenzi. "amesababisha watu kufikiri ya kwamba bikira wa Israeli ni mtu mbaya"

hatakiwi kumfukuza

"usimruhusu amuache"

katika siku zake zote

Hii ni lahaja. "katika maisha yake yote"

Deuteronomy 22:20

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Ila kama jambo hili ni la kweli

"Lakini kama ni kweli" au "Lakini kama kile ambacho mwanamume anasema ni kweli"

kwamba ushahidi wa bikira ya binti haukupatikana kwa binti

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ya kwamba mwanamume hakupata ushahidi ya kwamba binti alikuwa bikira"

ushahidi wa bikra

Nomino zinazojitegemea za "ushahidi" na "bikira" zinaweza kutafsiriwa kama misemo ya vitenzi. "kitu kinachothibitisha ya kwamba binti alikuwa bikira"

basi wanapaswa kumpeleka binti

"kisha wazee wanapaswa kumtoa binti nje"

kumpiga kwa mawe hadi afe

"kutupa mawe kwake mpaka afe"

kwa sababu amefanya jambo la aibu katika Israeli

"kwa sababu amefanya jambo la aibu katika Israeli"

kwa kutenda kama kahaba chini ya nyumba ya baba yake

"kutenda kama kahaba angali akiishi katika nyumba ya baba yake"

mtakuwa mmeondoa uovu

Kivumishi "uovu" kinaweza kutafsiriwa kama msemo wa nomino. "unapaswa kutoa miongoni mwa Waisraeli mtu ambaye anafanya jambo hili ovu" au "unapaswa kumuua mtu huyu muovu"

Deuteronomy 22:22

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza na Waisraeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo maneno "yako" hapa ni katika umoja.

Iwapo mwanamume kakutwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Kama mtu anamkuta mwanamume"

anyi mtakuwa mmeondoa

"kwa njia hii utakuwa umetoa"

Deuteronomy 22:23

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza na Waisraeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo maneno "yako" hapa ni katika umoja.

amechumbiwa na mwanamume

"'ambaye ameahidiwa kuolewa na mwanamume"

wachukueni ... kuwapiga mawe

Amri hizi zinatamkwa kwa Israeli kama kundi na kwa hiyo zipo katika wingi.

wachukueni wote wawili

"kisha unapaswa kuwaleta wote msichana na mwanamume aliyelala naye"

kwa sababu hakupaza sauti

"kwa sababu hakupaza sauti kuomba msaada"

kwa sababu amemwingilia mke wa jirani yake

Katika wakati huo Waisraeli walimchukulia mwanamume na mwanamke ambao walikuwa wamechumbiana kwa ajili ya ndia kama mume na mke. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "kwa sababu alilala na msichana ambaye alikuwa wa Muisraeli mwenzake"

nanyi mtakuwa mmeondoa uovu miongoni mwenu

Kivumishi cha "uovu" kinaweza kutafsiriwa kama msemo wa nomino. "unapaswa kuondoa miongoni mwa Israeli mtu ambaye anafanya jambo hili ovu" au "unapaswa kumuua mtu huyu muovu"

Deuteronomy 22:25

msichana aliyechumbiwa

Hii ina maana msichana ambaye wazazi wamekubali aolewe na mwanamume fulani, lakini msichana bado hajaolewa.

basi mwanamume pekee aliyelala naye ndiye lazima afe

"kisha unapaswa kumuua mwanamume tu ambaye alilala naye"

hakuna dhambi inayostahili kifo kwake msichana

"hautakiwi kumuadhibu kwa kumuua kwa kile alichofanya"

Kwa maana suala hili ni kama mwanamume amshambuliapo jirani yake na kumuua

"Kwa kwa sababu suala hili ni kama suala la mtu kumshambulia mtu mwingine na kumuua"

Kwa maana alimkuta shambani

"Kwa sababu mwanamume alimkuta msichana akifanya kazi shambani"

Deuteronomy 22:28

lakini hajachumbiwa

"lakini ambaye wazazi wake hawajamuahidi mwanamume mwingine ya kuwa ataolewa na yeye"

na kama wakagundulika

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "na kama mtu akagundua kilichotokea"

shekeli hamsini za fedha

Shekeli ina uzito wa gramu kumi na moja. "vipande hamsini vya fedha" au "gramu 550 za fedha"

Hatakiwi kumfukuza katika siku zake zote

Hii ni lahaja. "Hatakiwi kumpa talaka katika maisha yake yote"

Deuteronomy 22:30

hapaswi kumchukua mke wa baba yake kama wake

Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "hatakiwi kumuoa mke wa zamani wa baba yake, hata kama si mama yake"

Deuteronomy 23

Deuteronomy 23:1

Mwanamume aliyejeruhiwa kwa kupondwa au kukatwa

"mwanamume ambaye sehemu zake za siri zimepondwa au kukatwa"

kuingia katika kusanyiko la Yahwe

Hii ni lahaja. "anaweza kuwa mshiriki kamili wa jamii ya Israeli"

Mwana haramu

Maana zaweza kuwa 1) mtoto aliyezaliwa kwa wazazi ambao walijamiiana kwa maharimu au kuzini au 2) mtoto aliyezaliwa kwa kahaba.

kutoka hadi kizazi cha kumi cha uzao wake

Hii "kumi" ni nambari ya mpango ya kumi. "hata baada ya kizazi cha kumi cha vizazi vya mwana haramu"

hakuna kati yao

"hakuna kati ya vizazi hivi"

Deuteronomy 23:3

haruhusiwi kuwa miongoni mwa kusanyiko la Yahwe

Hii ni lahaja. "hawezi kuwa mshiriki kamili wa jamii ya Israeli"

kutoka hadi kizazi cha kumi cha uzao wake

Hii "kumi" ni mpangilio wa nambari kwa ajili ya kumi. "hata baada ya kizazi cha kumi cha uzao wake"

hawaku kutana nanyi kwa mkate na maji

Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "hawaku kukaribisha kwa kukuletea chakula na kinywaji"

dhidi yako ... awalaani

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika umoja.

Deuteronomy 23:5

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo maneno ya "wako" na "yako" hapa ni katika umoja.

hakumsikiliza

Hii ni lahaja. "hakuwa msikivu"

aligeuza laana kuwa baraka

"akamfanya ambariki na kutokulaani"

Hamtakiwi kutafuta amani au mafanikio yao

Maana zaweza kuwa 1) "Haupaswi kufanya makubaliano ya amani na Waamori na Wamoabu" au 2) "Haupaswi kufanya jambo lolote kusababisha masuala kwenda vizuri kwa yale makundi mawili ya watu kuwawezesha wafanikiwe"

katika siku zenu zote

Hii ni lahaja. "ikiwa bado wewe ni taifa"

Deuteronomy 23:7

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika umoja

Hutakiwi kumchukia Muedomi

"Usimchukie Muedomi"

kwa maana ni ndugu yako

"kwa sababu ni jamaa yako"

hutakiwi kumchukia Mmisri

"Usimchukie Mmisri"

Wazawa wa kizazi cha tatu wanaozaliwa kwao wanaweza kuwa katika kusanyiko la Yahwe

Hii "tatu" ni mpangilio wa nambari ya tatu. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "Kama Muedomi au Mmisri anakuja kuishi katika jamii ya Kiisraeli, wajukuu wake wanaweza kuwa washiriki kamili wa jamii"

Deuteronomy 23:9

Utakapotembea kijeshi dhidi ya maadui zako, basi unapaswa kujitenga

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika umoja.

dhidi ya maadui zako

"kupigana dhidi ya maadui zako"

kujitenga na kila aina ya uovu

"jitenge na mambo yote mabaya"

mwanamume ambaye sio msafi kwa sababu ya jambo lililofanyika kwake usiku

Hii ni njia ya upole ya kusema ya kwamba alikuwa na kutokwa kwa shahawa . "mwanamume yeyote ambaye ni mchafu kwa sababu alikuwa akitokwa na shahawa alipokuwa amelala"

Deuteronomy 23:12

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika umoja.

na utakuwa na kitu katika zana zako cha kuchimbia

"na unatakiwa kuwa na kifaa utakachotumia kuchimbia"

utakapochuchumaa kujisaidia

Hii ni njia ya upole ya kusema kunya. "unapochuchumaa chini kunya"

unapaswa kuchimbia nacho

"unapaswa kuchimba shimo kwa kifaa"

kufunika kile kilichotoka kwako

"funika kinyesi chako"

ili kwamba asione kitu chochote kichafu miongoni mwenu

"ili kwamba Yahwe asione kitu chochote kichafu miongoni mwenu"

Deuteronomy 23:15

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika umoja.

mtumwa aliyetoroka kwa bwana wake

Maana kamili inaweza kuwekwa wazi. "mtumwa kutoka katika nchi nyingine aliyetoroka kwa bwana wake na kuja Israeli"

Mruhusu aishi pamoja nawe

"Mruhusu mtumwa kusihi miongoni mwa watu wenu"

Deuteronomy 23:17

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "wako" hapa ni katika umoja.

kahaba wa kidini ... kahaba wa kidini ... kahaba ... mbwa

Yahwe anatoa orodha kamili ya aina mbili za ukahaba za wanamume na wanawake kukataza ukahaba wa mtu kwa sababu yoyote ile.

kahaba wa kidini ... miongoni mwa mabinti ... miongoni mwa wana wa kiume

Maana zaweza kuwa ya kwamba Musa 1) alikataza wazi wanawake na wanamume kufanya matendo ya ngono kama sehemu ya ibaada hekaluni au 2) anatumia tasifida kukataza wanawake na wanamume kufanya matendo ya ngono kupokea pesa.

Hautakiwi kuleta mshahara wa kahaba ... katika nyumba

"Mwanamke anayepata pesa kama kahaba hatakiwi kuleta pesa hiyo ... katika nyumba"

mbwa

mwanamume ambaye anaruhusu wanamume kufanya ngono na yeye kwa pesa

katika nyumba ya Yahwe Mungu wako

"katika hekalu"

kwa kiapo chochote

"kutimiza kiapo"

vyote hivi

mshahara wa kahaba wa kike na kahaba wa kiume.

Deuteronomy 23:19

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "wako" hapa ni katika umoja.

Hutakiwi kumkopesha Muisraeli mwenzako kwa riba

"Kama utakopesha kitu kwa Muisraeli mwenzako, hautakiwi kumfanya alipe zaidi ya alivyokopa"

kukopesha kwa riba

kumkopesha mtu na kumlazimisha mtu huyo kulipa zaidi ya kile alichokopa

riba ya fedha ... kitu chochote kinachokopeshwa kwa riba

"hautakiwi kulipiza riba unapomkopesha mtu pesa, chakula, au kitu chochote"

kila jambo uwekalo mkono wako

Hii ni lahaja. "kila unachofanya"

Deuteronomy 23:21

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo maneno "kwako" na "wako" hapa ni katika umoja.

haupaswi kukawia kuikamilisha

"hautakiwi kutumia muda mrefu kukamilisha kiapo hiki"

maana Yahwe Mungu wako hakika atadai kiapo hicho

"kwa sababu Yahwe Mungu wako atakulaumu na kukuadhibu iwapo hautakamilisha kiapo chako"

Lakini iwapo utajizuia kutoa kiapo, haitakuwa dhambi kwako

Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "Lakini, kama hautatoa kiapo, hautakuwa umetenda dhambi kwa sababu hautakuwa na kiapo cha kutimiza"

Kile ambacho kimetoka kinywani mwako

Hii ni lahaja. "Maneno uliyozungumza"

kulingana na kiapo ulichotamka kwa Yahwe Mungu wako

"chochote ulichoapa kwa Yahwe Mungu wako ambacho utafanya"

chochote ulichotamka kwa hiari kwa kinywa chako

"chochote ambacho watu wamesikia ukiahidi kufanya kwa sababu ulitaka kukifanya"

kinywa chako

"ili kwamba watu wasikie ukikitamka"

Deuteronomy 23:24

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo maneno ya "wako" na "yako" hapa ni katika umoja.

unaweza kula mizabibu idadi yoyote unayotaka

"kisha unaweza kufurahia kula mizabibu mpaka utosheke"

lakini usiweke yoyote katika kikapu chako

Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "lakini haupaswi kuweka mizabibu yoyote katika kikapu chako kubeba pamoja nayo"

Utakapokwenda katika shamba la zao lililoiva la jirani yako

"Utakapokwenda katika shamba la jirani yako ambapo kuna zao linaota"

unaweza kuvuna kichwa cha mavuno kwa mkono wako

"kisha unaweza kula viini vya mbegu kwa mikono yako"

lakini haupaswi kutumia mundu kuvuna zao lililoiva la jirani yako

"lakini usikate chini mazao yalioiva ya jirani yako na kuchukua"

mundu

kifaa chenye ncha kali ambacho wakulima hutumia kuvuna ngano

Deuteronomy 24

Deuteronomy 24:1

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Mwanamume akimchukua mke na kumuoa

Misemo "kuchukua mke" na "kumuoa" ina maana moja. "Mwanamume anapomuoa mwanamke"

asipokubalika machoni pa mumewe

Hapa "machoni pake" ina maana ya mtu mzima. "akiamua ya kwamba hampendi"

kwa sababu kagundua jambo ambalo si jema kwake

"kwa sababu fulani ameamua ya kwamba hataki kukaa naye"

anatakiwa amwandikie talaka

"anapaswa kumpa mke wake karatasi rasmi inayosema ya kwamba hawajoana tena"

anaweza kwenda na kuwa mke wa mwanamume mwingine

"anaweza kuondoka na kuolewa na mwanamume mwingine"

Deuteronomy 24:3

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli juu ya mwanamume anayepata talaka na kuoa mwanamume mwingine.

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika umoja.

Iwapo mume wa pili akamchukia

"Kama mume wa pili akaamua ya kwamba anamchukia mwanamke huyu"

talaka

Hii ni karatasi rasmi inayosema ya kwamba mwanamume na mwanamke hawajaoana tena.

akaiweka mkononi mwake

"kumpatia mwanamke"

mwanamume aliyemchukua kuwa mke wake

"mwanamume wa pili aliyemuoa mwanamke"

baada ya yeye kuwa mchafu

Maana kamili ya kauli hii inawez akuwekwa wazi. "baada ya kuwa mchafu kwa talak na ndoa nyingine kwa mwanamume mwingine"

Hautakiwi kusababisha nchi iwe na hatia

Nchi inazungumziwa kana kwamba inaweza kutenda dhambi. "hautakiwi kusambaza hatia katika nchi"

Deuteronomy 24:5

Taarifa ya Jumla:

Musa bado anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Mwanamume atakapochukua mke mpya

"Mwanamume anapokuwa ameoa mke mpya"

na wala hataamrishwa kwenda kwenye shughuli yoyote ya kulazimishwa

Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "na hakuna mtu wa kumlazimisha kuishi mbali na nyumba yake na kufanya aina yoyote ya kazi"

atakuwa huru kuwa nyumbani

"atakuwa huru kuishi nyumbani"

Deuteronomy 24:6

kinu

kifaa kinachotumika kutengeneza unga kwa kusaga mbegu katikati ya mawe mawili mazito.

jiwe la kinu

sehemu ya juu ya jiwe katika kinu

kwa maana hivyo itakuwa kuchukua maisha ya mtu kama dhamana

Neno "maisha" ni lugha nyingine ya kile mtu anachohitaji kuweza kuishi. "kwa sababu atakuwa amechukua kutoka kwa mtu kile ambacho mtu anahitaji kutengeneza chakula kwa ajili ya familia yake"

Deuteronomy 24:7

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika umoja.

Iwapo mwanamume kakutwa kamteka

Hii ni lahaja kwa ajili ya "Kama mwanamume anamteka". Inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "kama utamkuta mwanamume amemteka"

kamteka

kutumia nguvu kwa lazima kumchukua mtu asiye na hatia kutoka nyumbani kwake na kumfunga mateka

moja wa kaka zake miongoni mwa watu wa Israeli

"moja kati ya Waisraeli wenzake"

huyo mwizi lazima afe

"kisha Waisraeli wengine wanapaswa kumuua mwizi huyo kama adhabu ya kile alichofanya"

na utakuwa umeondoa uovu miongoni mwenu

Kivumishi cha "uovu" kinaweza kutafsiriwa kama kitenzi. "na unatakiwa kumtoa miongoni mwa Waisraeli mtu anayefanya uovu huu" au "nawe unapaswa kumuua mtu huyu muovu"

Deuteronomy 24:8

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Kuwa mwangalifu ... makini katika kuchunguza ... Kumbukeni nini Yahwe Mungu wako

Musa anazungumza na Waisraeli hapa kana kwamaba wao ni mtu mmoja, kwa hiyo neno "wako" na amri "kuwa mwangalifu" na "kumbukeni" ni katika umoja.

Kuwa mwangalifu kuhusu kiini chochote cha ukoma

"kuwa makini iwapo utapata ukoma" au "Kuwa makini kama utakuwa na ukoma"

kila agizo linalopewa kwako ambalo makuhani, Walawi, wanakufundisha

Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "maagizo yote ambayo nimekupatia na ambayo makuhani, ambao ni Walawi, wanakufundisha kufanya"

wanakufundisha ... utekeleze ... ulipokuwa ukitoka

Musa hapa anazungumza na Waisraeli kama kikundi kwa hiyo maneno "ukitoka" ni katika wingi.

kama nilivyowaamuru, ili utekeleze

"unapaswa kuhakikisha ya kwamba unafanya kama nilivyowaamuru wao"

nilivyowaamuru

Neno la "wao" lina maana ya makuhani, ambao ni makuhani.

Kumbukeni

Hii ni lahaja. "Kumbuka"

ulipokuwa ukitoka Misri

"katika kipindi ambacho ulikuwa unaondoka Misri"

Deuteronomy 24:10

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza na Waisraeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" na "wako" hapa ni katika umoja.

Utoapo mkopo wa aina yoyote kwa jirani yako

"Unapotoa mkpo wa kitu kwa jirani yako"

kutafuta dhamana yake

"kuchukua dhamana yake"

dhamana yake

Hii ni lugha nyingine ya "kile alichoahidi angefanya kutoa kama angeshindwa kulipa kile alichokopa"

Utasimama nje

"unatakiwa kusubiri nje ya nyumba"

Deuteronomy 24:12

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika umoja.

hautakiwi kulala na dhamana yake ikiwa mikononi mwako

"Hautakiwi kubaki na koti lake usiku wote"

dhamana yake

Hii ni lugha nyingine ya "kile alichoahidi angefanya kutoa kama angeshindwa kulipa kile alichokopa"

kumrejeshea dhamana yake

"umrudishie alichokupatia kukuonyesha ya kwamba atalipa mkopo wake"

ili aweze kulala ndani ya vazi lake na akubariki

Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "ili kwamba aweze kuwa na koti lake kujipatia joto anapolala, na kuwa na shukurani kwako"

vazi

Koti au nguo nyingine ambayo humpatia mtu joto wakati wa usiku. Yawezekana hii ilikuwa "dhamana" ambayo Musa alikuwa akizungumzia katika 24:10.

itakuwa utakatifu kwako mbele za Yahwe Mungu wako

"Yahwe Mungu wako atatoa kibali kwa jinsi ulivyosimamia suala hili"

Deuteronomy 24:14

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo maneno "yako" na "wako" hapa ni katika umoja.

Hautakiwi kumuonea mtumishi wa kuajiriwa

"Hautakiwi kumtendea mtumishi wa kuajiriwa vibaya"

mtumishi wa kuajiriwa

mtu ambaye hulipwa kila siku kwa kazi yake

maskini na muhitaji

Maneno haya mawili yana maana za kufanana na husisitiza ya kwamba mtu huyu hawezi kujisaidia mwenyewe.

ndani ya malango ya mji wako

Hapa "malango ya mji" ina maana ya miji au mjini. "moja ya miji yenu"

Kila siku unapaswa kumlipa mshahara wake

"Unapaswa kumpatia mwanamume pesa anayopata kila siku"

jua halipaswi kuzama kabla ya suala hili kutatuliwa

Hii ni lahaja. Waisraeli walichukulia siku mpya kuanza pale jua linapozama. "unatakiwa kumlipa mtu katika siku hiyo anayofanya kazi"

kwa maana ni maskini na anautegemea

Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "kwa sababu ni maskini na anategemea mshahara wake kununua chakula chake cha siku inayofuata"

asilie dhidi yako kwa Yahwe

"asipaze sauti kwa Yawhe na kumuomba akuadhibu"

Deuteronomy 24:16

Wazazi hawapaswi kuuwawa kwa niaba ya watoto wao

Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "Haupaswi kuwaua wazazi kwa sababu ya jambo baya ambalo mmoja wa watoto wamefanya"

na wala watoto hawapaswi kuuawa kwa niaba ya wazazi wao

Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "na haupaswi kuwaua watoto kwa sababu ya jambo baya ambalo wazazi wao wamefanya"

kila mtu anapaswa kuuwawa kwa dhambi yake mwenyewe

Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "unapaswa kumuua mtu kwa sababa ya jambo baya alilofanya mwenyewe tu"

Deuteronomy 24:17

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "wako" hapa ni katika umoja.

Haupaswi kutumia nguvu kuchukua haki inayomhusu mgeni au yatima

Musa anazungumzia haki kana kwamba ilikuwa kitu halisi ambacho mtu mwenye nguzu zaidi anaweza kukivuta kwa nguvu kutoka kwa mtu mnyonge. "Haupaswi kumtendea mgeni au yatima kinyume na haki"

yatima

Hii ina maana ya watoto ambao wazazi wote wamefariki na hawana ndugu wa kuwatunza.

wala kuchukua vazi la mjane kama dhamana

Mkopeshaji huchukua kitu kutoka kwa mkopaji kuhakikisha ya kuwa angewez kumlipa. Hakuruhusiwa kuchukua vazi lake kwa maana alihitaji kumpatia joto. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "na usichukue vazi la mjane kama dhamana kwa sababu anahitaji kuwa na joto"

ukumbuke

Hii ni lahaja. "kumbuka"

Deuteronomy 24:19

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika umoja.

Utakapovuna zao lako shambani mwako

"Utakapokata zao la shamba lako"

tita

mazao ambayo mvunaji amezifunga pamoja

kinapaswa kuwa cha mgeni, cha yatima, au cha mjane

Unaweza kufanya taarifa ieleweke. "unatakiwa kubakia tita ili kwamba mgeni, na yatima, au mjane anaweza kuchukua"

katika kazi ya mikono yako

Hapa "mikono" ina maana ya mtu mzima. "katika kazi yako yote unayofanya"

Utakapotikisa mti wako wa mzeituni

Unaweza kufanya taarifa ieleweke. "Unapotikisa matawi ya mti wa mzeituni, kusababisha mzeituni kuanguka kwenye nchi ili uweze kuchukua"

haupaswi kupanda juu ya matawi tena

"usiokote kila tawi moja kutoka kwenye mti"

itakuwa kwa ajili ya mgeni, kwa yatima na kwa mjane

Unaweza kufanya taarifa ieleweke. "mizeituni inayobaki katika matawi ni kwa ajili ya wageni, yatima, na wajane kuokota na kuondoka navyo"

Deuteronomy 24:21

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika umoja.

kitakuwa cha mgeni, cha yatima na cha mjane

"mizabibu ambayo hautaokota itakuwa kwa ajili ya mgeni, yatima, na mjane kuokota"

cha mgeni, cha yatima na cha mjane

Hii ina maana yamakundi ya watu. "kwa ajili ya wageni, kwa wale yatima, au kwa wajane"

ukumbuke

Hii ni lahaja. "kumbuka"

Deuteronomy 25

Deuteronomy 25:1

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Iwapo mwanamume mwenye hatia anastahili kupigwa

Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "Kama muamuzi ataamuru wampige mtu mwenye hatia"

na kupigwa mbele zake

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "na atawatazama wakimpiga"

kwa idadi iliyoamriwa kulingana na kosa lake

"idadi ya namba aliyoamuru kwa sababu ya matendo mabaya aliyoyafanya"

Deuteronomy 25:3

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Muamuzi anaweza kumpatia mapigo arobaini

"Muamuzi anaweza kusema ya kwamba wanatakiwa kumpiga mtu mwenye hatia mara 40"

lakini hapaswi kuvuka idadi hiyo

"lakini muamuzi hapaswi kuwaamuru wampige zaidi ya mara 40"

kwa maana akivuka idadi hiyo na kumpiga kwa mapigo mengi zaidi

"kwa sababu kama muamuzi atawaamuru kumpiga zaidi ya mara 40"

basi Muisraeli mwenzako atakuwa kaaibishwa mbele ya macho yenu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "kisha muamuzi atamuaibisha Muisraeli mwenzako mbele ya watu wote wa Israeli"

kaaibishwa mbele ya macho yenu

Hapa lugha nyinginr ya "mbele ya macho yenu" ina maana ya kile watakachokiona. "kuaibishwa, nanyi wote mtaona". Maneno ya kufanana hujitokeza katika 1:7

Deuteronomy 25:4

Haupaswi kumfunga punda

"Hautakiwi kuweka kitu kwenye mdomo wa punda"

anapokuwa akilima shamba

wakati akitenganisha mazao na makapi kwa kutembea juu yake au kuburuza mbao nzito juu yake

Deuteronomy 25:5

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Iwapo kaka wanaishi pamoja

Maana zaweza kuwa 1) "kama ndugu wanaishi katika mahali pamoja" au 2) "kama ndugu wanaishi karibu na mwenzake".

basi mke wa marehemu hatakiwi kuolewa na mtu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "kisha familia ya mtu aliyekufa anapaswa kumruhusu mjane aolewe na mtu"

na kutekeleza wajibu wa kaka wa mume kwake

"na kufanya kile ambacho kaka wa mume aliyefariki anatakiwa kufanya"

atarithi chini ya jina la kaka yake mwanamume aliyefariki

Neno "jina" ni lugha nyingine ya ukoo wa mtu. "ataendeleza ukoo wa kaka wa mtu aliyekufa"

ili jina lake lisiangamie ndani ya Israeli

Neno "jina" ni lugha nyingine ya ukoo wa mtu. "ili kwamba ukoo wake usipotee kutoka Israeli"

Deuteronomy 25:7

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

napaswa kwenda malangoni mpaka kwa wazee

Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "unapaswa kwenda juu katika malango ya mji ambapo wazee huamua masuala"

amekataa kuwajibika kwa niaba ya jina la kaka yake

Hapa "jina" ina maana ya kumbukumbu ya mtu kupitia uzao wake. "anakataa kumpatia kaka yake mwana"

hataki kufanya wajibu wa kaka wa mume kwangu

"hatafanya kile ambacho kaka wa mume wake anatakiwa kufanya na kunioa"

Sitaki kumchukua

"Sitaki kumuoa yeye"

Deuteronomy 25:9

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

anatakiwa kuja kwake mbele ya wazee

"anapaswa kutembea kwake huku wazee wakimuangalia"

asiyetaka kujenga nyumba ya kaka yake

Hapa "nyumba" ni lugha nyingine ya familia. "ambaye hampatii kaka yake mwana na kuendeleza ukoo wa kaka yake"

Jina lake Israeli litaitwa

"Watu wa Israeli watajua familia yake kama"

Nyumba ya mtu aliyevuliwa ndara zake

Hapa kutoa ndara inaashiria ya kwamba kaka asingepokea mali yoyote ya kaka yake aliyefariki. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Nyumba ya yule ambaye ndara yake ilivuliwa na mjane wa kaka yake aliyekufa ambaye hakumuoa" au "familia ambayo kila mtu anaichukia" au "Familia ambayo ni ya aibu"

Deuteronomy 25:11

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "lako" hapa ni katika umoja.

kutoka mikononi mwa yule aliyempiga

Hapa "mkono" una maana ya nguvu au utawala. "kwa hiyo yule aliyempiga hatampiga tena" au "kutoka kwa mwanamume aliyempiga"

jicho lako halipaswi kuwa na huruma

Hapa "jicho" lina maana ya mtu mzima. "hautakiwi kumhurumia" au "hautakiwi kuonyesha huruma kwake"

Deuteronomy 25:13

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika umoja.

Haupaswi kuwa na mizani ya uzito tofauti katika mfuko wako, mkubwa na mdogo

Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. Unaweza kuweka wazi taarifa inayoeleweka. "Hautakiwi kudanganya watu kwa kutumia uzito ambao ni mkubwa kuliko jinsi ulivyosema ulikuwa unaponunua vitu na kwa kutumia uzito ambao ni mdogo zaidi ya ulivyosema ulikuwa unapouza vitu"

mizani

Mizani ni mawe yanayotumika juu ya usawa kuthibitisha jinsi gani kitu kina uzito

Hautakiwi kuwa na vipimo tofauti ndani ya nyumba yako, vikubwa na vidogo

Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. Unaweza kuweka wazi taarifa inayoeleweka. "Hautakiwi kudanganya watu kwa kutumia uzito ambao ni mkubwa kuliko jinsi ulivyosema ulikuwa unaponunua vitu na kwa kutumia uzito ambao ni mdogo zaidi ya ulivyosema ulikuwa unapouza vitu"

vipimo

Kipimo kilikuwa kikapu au chombo kingine cha kupimia jinsi gani kitu kilikuwa na ujazo.

Deuteronomy 25:15

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba alikuwa akizungumza na mtu mmoja, kwa hiyo maneno "zako" na "wako" ni katika umoja.

kamili na wa haki

"sahihi na haki"

uzito ... vipimo

Uzito ni mawe yanayotumika juu ya usawa kuthibitisha jinsi gani kitu kina uzito. Kipimo kilikuwa kikapu au chombo kingine cha kupimia jinsi gani kitu kilikuwa na ujazo.

siku zako ziwe ndefu

Hii ni lahaja. "unaweza kuishi kwa muda mrefu"

Kwa maana wote wanaofanya vitu hivi, wote wanaovunja haki

"kwa sababu kila mtu anayedanganya watu kwa kutumia ukubwa tofauti wa uzito na vipimo.

Deuteronomy 25:17

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika umoja.

Kumbuka ni jambo gani Amaleki alichofanya kwako

Hii ni lahaja, na "Amaleki" ni lugha nyingine kwa ajili ya watu wa Amaleki. "Kumbukeni kile Waamaleki walichowafanyia"

ulipokuwa ukitoka

Neno "ukitoka" hapa ni katika wingi.

jinsi alivyokutana na wewe barabarani

"jinsi walivyokutana na wewe njiani"

na kuwashambulia kati yenu kwa nyuma

"na kushambulia wale watu wenu waliokuwa mstari wa nyuma"

wale waliokuwa wamelegea nyuma

"watu wote waliokuwa dhaifu nyuma ya mstari"

dhaifu na kuchoka

Maneno haya yana maana moja na yanasisitiza jinsi watu walivyokuwa wamechoka. "kuchoka na kuchoka kabisa"

hakumheshimu Mungu

Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "hakuwa anaogopa adhabu ya Mungu" au "hakumheshimu Mungu"

unapaswa kufuta kumbukumbu ya Waamaleki chini ya mbingu

"unatakiwa kuwaua Waamaleki wote ili kwamba hakuna yeyote atakayewakumbuka tena"

Deuteronomy 26

Deuteronomy 26:1

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza na Waisraeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika umoja.

baadhi ya mavuno yote ya kwanza

"baadhi ya matunda ya kwanza ya mavuno" au "baadhi ya mazao ya kwanza ya mavuno". Hii "kwanza" ni mpangilio wa nambari ya moja.

Deuteronomy 26:3

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza na Waisraeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "wako" hapa ni katika umoja.

Deuteronomy 26:5

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza na Waisraeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "wako" hapa ni katika umoja.

Babu yangu alikuwa Mwaremi mzururaji

Huu ni mwanzo wa kauli ya kwamba mwanamume wa Kiisraeli anatakiwa kutengeneza anapoleta kikapu chake.

Mwaremi mzururaji

Hii ina maana ya Yakobo, ambaye alikuwa baba wa Waisraeli wote. Aliishi miaka mingi katika Aramu-Nahairamu, eneo lililopo Shamu.

na kukaa kule

"na kuishi maisha yake yote kule"

Kule akawa

Neno "akawa" ni lugha nyingine kwa ajili ya "uzao wa Yakobo"

kubwa, lenye nguvu

Maneno haya kimsingi yana maana moja. Yanasisitiza ya kwamba Israeli ikawa taifa kubwa na lenye nguvu. "kubwa sana"

Deuteronomy 26:6

Taarifa ya Jumla:

Hii inaendeleza kile Muisraeli anapswa kulema anapoleta mazao yake ya kwanza kwa Yahwe.

walitutendea vibaya na kututesa

Misemo hii miwili kimsingi inasema kitu kimoja. Inasisitiza ya kwamba Wamisri walitenda kwa ukatili sana.

walitutendea

Hapa "walitutendea" ina maana ya watu wa Israeli ambao walikuwa wakiishi Misri. Mwandishi anajijumuisha mwenyewe kama mmoja wa watu hata kama aliishi Misri au la.

akasikia sauti yetu

Hapa "sauti" ina maana ya mtu mzima na kilio au maombi yake. "alisikia vilio vyetu" au "alisikia maombi yetu"

mateso yetu, kazi zetu na mateso yetu

"ya kwamba Wamisri walikuwa wakitutesa, ya kwamba tulikuwa tukifanya kazi ngumu sana, na kwamba Wamisri walikuwa wakitutesa"

Deuteronomy 26:8

Taarifa ya Jumla:

Hii inaendeleza kile ambacho Muisraeli anatakiwa kusema pale anapoleta mazao yake ya kwanza kwa Yahwe.

Yahwe alituondoa

Hapa "alituondoa" ina maana ya watu wa Israeli ambao walikuwa wakiishi Misri. Mwandishi anajijumlisha mwenyewe kama mmoja wa watu hata kama aliishi Misri au la.

kwa mkono wake mkuu, kwa mkono wake ulionyoshwa

Hapa "mkono mkuu" na "mkono ulionyoka" ni sitiari kwa nguvu ya Yahwe. "kwa kuonyesha nguvu yake" Maneno kama haya hujitokeza katika 4:34.

kwa hofu kuu

"kwa matendo ambayo yaliwatisha watu waliyoyaona"

nchi inayotiririka kwa maziwa na asali

Hii ni lahaja. "nchi yenye maziwa mengi na mtiririko wa asali" au "nchi ambayo inafaa kwa mifugo na ukulima"

Deuteronomy 26:10

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuwaambia Waisraeli kile wanachotakiwa kusema pale watakapoleta mazao yao ya kwanza kwa Yahwe. Anazungumza kwao kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "wako" na "yako" hapa ni katika umoja.

mavuno ya kwanza

"matunda ya kwanza ya mavuno" au "mazao ya kwanza ya mavuno"

Unapaswa kuweka chini

"Unapaswa kuweka kikapu chini"

unapaswa kufurahia katika mema yote ambayo Yahwe Mungu wako amekufanyia

"unapaswa kufurahi na kushukuru kwa mambo yote mazuri ambayo Yahwe Mungu wako amekufanyia"

Deuteronomy 26:12

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza na Waisraeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "wako" na "yako" hapa ni katika umoja.

katika mwaka wa tatu

Hapa "tatu" ni mpangilio wa nambari ya tatu. Kila miaka mitatu watu wa Israeli walitoa moja ya kumi ya mavuno kwa maskini.

yatima

Hawa ni watoto ambao wazazi wao wote wamefariki na hawana jamaa wa kuwatunza.

mjane

Hii ina maana mwanamke ambaye mume wake amefariki na hana watoto wa kumtunza sasa akiwa mzee.

kula ndani ya malango yenu ya mji na kujazilishwa

Hapa "malango" ina maana ya miji au mji. "ili kwamba wale wanaoishi ndani ya miji yenu wawe na chakula cha kutosha kwa kula"

Nimetoa kutoka

Haya ni maneno ya kwanza ya kauli nyingine ambayo Muisraeli alitakiwa kusema.

wala sijazisahau.

Hii ina maana ya kwamba ametii amri zote za Mungu.

Deuteronomy 26:14

Taarifa ya Jumla:

Hii inaendeleza kile ambacho Muisraeli anapaswa kusema kwa Yahwe anapotoa zaka yake kwa maskini.

Sijala kati yao wakati wa maombolezo yangu

"Sijala chochote katika zaka nilipokuwa nikiomboleza"

nilipokuwa mchafu

Hapa "mchafu" ina maana ya mtu ambaye sio msafi kulingana na Sheria. Mungu haruhusu mtu aliye mchafu kugusa zaka anayotoa kwa Mungu. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "nilipokuwa mchafu kulingana na Sheria" au "sheria inaposema siwezi kuigusa"

Nimesikiliza sauti ya Yahwe Mungu wangu; Nimetii kila kitu ulichoniamuru kukifanya

Hapa "sauti ya Yahwe" ni lugha nyingine kwa kile Yahwe alichosema. Kauli hizi mbili zinatumia maana moja. Zinasisitiza ya kwamba mtu ametii amri zote za Mungu.

kutoka mahali patakatifu unapoishi, kutoka mbinguni

Misemo hii miwili ina maana moja. "kutoka mbinguni, sehemu yako takatifu"

nchi inayotiririka kwa maziwa na asali.

Hii ni lahaja. "nchi ambapo kuna maziwa na asali inayotiririka" au "nchi ambayo inafaa sana kwa mifugo na kilimo"

Deuteronomy 26:16

Taarifa ya Jumla

Musa anazungumza na Waisraeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika umoja.

kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote

Lahaja ya "kwa moyo wako" ina maana "kikamilifu" na "kwa nafsi yote" ina maana ya "nafsi yako yote". Misemo hii miwili ina maana moja. "kwa nafsi yako yote" au "kwa nguvu zako zote".

kwamba utatembea katika njia zake na kushikilia sheria zake, maagizo yake na amri zake, na kwamba utaisikiliza sauti yake

Maneno "utatembea", "kushikilia", na "utasikiliza" ina maana ya kufanana hapa. Hapa "sauti" ina maana ya kile Mungu alichosema. "ya kwamba utatii kikamilifu kila kitu Yahwe anachoamuru"

Deuteronomy 26:18

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "wako" hapa ni katika umoja.

watu ambao ni mali yake

"watu ambao ni wa kwake"

atawaweka juu zaidi

Hii ni lahaja. "atakufanya uwe wa muhimu zaidi kuliko" au "atakufanya uwe mkubwa zaidi ya"

atawaweka juu zaidi ya mataifa mengine aliyoyaumba nanyi mtapokea sifa, umaarufu na heshima

Maana zaweza kuwa 1) "atakusababisha uwe mkubwa kuliko taifa lingine lolote ambalo ameimarisha, naye atakuwezesha kumsifu na kumheshimu" au 2) "atakuwa na watu wakimsifu zaidi ya jinsi wanavyosifu taifa lingine ambalo alifanya; watu watasema ya kwamba wewe ni bora zaidi ya taifa lingine, nawe watakuheshimu"

Mtakuwa watu waliowekwa kando kwa Yahwe Mungu wako

Yahwe kuchagua watu wa Israeli wawe wake ni njia maalumu ambayo inazungumziwa kana kwamba Yahwe aliwaweka kando kutoka kwa matiafa mengine. Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "Yahwe Mungu wako atakuweka kando kutoka kwa mataifa mengine"

Deuteronomy 27

Deuteronomy 27:1

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza na Waisraeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo isipokuwa, maneno "yake" ni katika umoja.

ninazowaamuru leo ... mtakapopita

Musa anazungumza na Waisraeli kama kundi, kwa hiyo sehemu zote mbili za neno "wako" ni katika wingi.

ninazowaamuru

Hapa "ninazowaamuru" ina maana ya Musa. Wazee wapo pale kwa makubaliano na Musa, lakini ni yeye peke yake anayezungumza.

kuyachapa kwa lipu

Lipu mara kwa mara ni mchanganyiko wa chokaa, mchanga, na maji ambazo husambazwa juu ya kitu.

nchi inayotiririka kwa maziwa na asali

Hii ni lahaja. "nchi ambayo maziwa mengi na asali hutiririka" au "nchi ambayo ni sahihi kwa mifugo na kilimo"

Deuteronomy 27:4

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza na Waisraeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "wako" hapa ni katika umoja.

Mtakapovuka ... yapangane ... ninayowaamuru

Musa anawataarifu Waisraeli kama kundi, kwa hiyo sehemu za "wako" na amri "yapangane" ni katika wingi.

myapige kwa lipu

"sambaza lipu juu yao" au "zitengeneze ili kwamba uweze kuandika juu yao"

mlima wa Ebali

Huu ni mlima karibu na Shekemu.

hautakiwi kuinua chombo cha chuma kujenga mawe

Hii ina maana ya patasi ambayo zingetengeneza mawe kuwa laini, ili yaweze kutosha pamoja vizuri zaidi. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "hautachonga mawe ya madhabahu kwa vifaa vya chuma"

Deuteronomy 27:6

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "wako" hapa ni katika umoja.

mawe yasiyokuwa na kazi

mawe yaliyo katika maumbo yao ya asili ambayo hakuna mtu aliyeyachonga kwa vifaa vya chuma

Utaandika juu ya mawe

Hii ina maana ya mawe yaliyowekwa juu ya mlima wa Ebali na kufunikwa kwa lipu.

Deuteronomy 27:9

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika umoja.

utii sauti ya Yahwe Mungu wako

Hapa lugha nyingine ya "sauti ya Yahwe" ina maana ya kile anachosema. "tii kile Yahwe Mungu wako anachosema"

ninawaamuru

Musa anawaamuru. Walawi wapo pale kukubaliana na Musa, lakini ni yeye peke yake anayezungumza.

Deuteronomy 27:11

Makabila haya

Hapa lugha nyingine ya "makabila" ina maana ya watu kutoka kwa makabila ya Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Yusufu, na Benyamini. "Watu kutoka kwa makabila haya"

mlima Gerizimu

Mlima mdogo kaskazini mwa Mlima Ebali.

Yusufu

Hii inajumlisha makabila ya Efraimu na Manase, ambao ni vizazi vya Yusufu.

Deuteronomy 27:13

mlima Ebali

Haya ni maneno ya milima iliyo upande wa magharibi wa Mto Yordani.

kutamka laana

"kusema kwa sauti kuu jinsi Yahwe atakavyokulaani Israeli"

Deuteronomy 27:15

Alaaniwe mwanamume ... ataifanya sirini

Hii ni kauli ambayo Walawi wanapaswa kupaza sauti kwa watu wote wa Israeli. Inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "Yahwe na alaani mtu ... kuwekwa kando sirini"

kazi ya mikono ya fundi

Hii ni lahaja. "jambo ambalo mtu amefanya"

fundi

mwanamume ambaye anajua kufanya mambo yawe bora

Deuteronomy 27:16

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuwaambia Walawi na watu kile wanachopaswa kusema.

Alaaniwe mwanamume

Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "Na Yahwe na alaani mwanamume"

anayetoa alama ya ardhi ya jirani yake

Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "ambaye anachukua ardhi kutoka kwa jirani yake kwa kutoa alama za mipaka ya ardhi yake"

Deuteronomy 27:18

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuwaambia Walawi na watu kile wanachopaswa kusema.

Alaaniwe mwanamume

Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "Na Yahwe alaani mwanamume"

atumiaye nguvu kupokonya haki inayomstahili mgeni ... mjane

Musa anazungumzia haki kana kwamba ilikuwa kitu halisia ambayo mtu mwenye nguvu anaweza kuvuta kwa nguvu kutoka kwa mtu dhaifu. Lugha yako inaweza kuwa na neno moja yenye maana "kutumia nguvu kuchukua". Maana zingine zinajitokeza katika 24:17."kumtendea mgeni ... mjane bila haki"

yatima

Hawa ni watoto ambao wazazi wake wawili wamefariki na hawana jamaa wa kuwatunza.

mjane

Hii ina maana ya mwanamke ambaye mume wake amefariki na hana watoto ambao wanamtunza katika uzee wake.

Deuteronomy 27:20

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuwaambia Walawi na watu kile wanachotakiwa kusema.

Alaaniwe mwanamume

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Na Yahwe amlaani mtu"

mke wa baba yake

Hii haimaanishi mama wa mwanamume, lakini mke mwingine wa baba yake.

amechukua haki za baba yake

Mwanamume anapomuoa mwanamke, ni yeye pekee ana haki halali ya kulala naye. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "amechukua haki halali za baba yake"

atakayelala na aina yoyote ya mnyama

Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "anayelala na aina yoyote ya mnyama kwa namna ambayo mwanamume hulala na mwanamke"

Deuteronomy 27:22

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuwaambia Walawi na watu kile wanachotakiwa kusema.

Alaaniwe mwanamume

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "na Yahwe amlaani mtu"

binti wa baba yake, au binti wa mama yake

Hii ina maana mwanamume hatakiwi kulala na dada yake, hata kama ana mama au baba tofauti.

Deuteronomy 27:24

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuwaambia Walawi na watu kile wanachotakiwa kusema.

Alaaniwe mwanamume

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "na Yahwe amlaani mtu

Deuteronomy 27:26

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuwaambia Walawi na watu kile wanachotakiwa kusema

Alaaniwe mwanamume

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "na Yahwe amlaani mtu

Deuteronomy 28

Deuteronomy 28:1

Habari ya jumla

Musa uzungumza na Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo maneno "wewe" na "wako" hapa ni umoja

kwa sauti ya Yahwe Mungu wako

Hapa maneno "sauti ya Yahwe" urejea kwa kile asemavyo. "Kwa kile Yahwe Mungu wenu asemavyo"

ili kushika

"na kutii"

jiweke juu

Musa uzungumza kuwa muhimu au kuwa kuu kama ilikuwa kubwa kimwili, kama juu ya mlima."kukufanya wewe muhimu zaidi kuliko" au kukufanya wewe mkuu kuliko"

Baraka hizo zote zitakuwa kwako na kukupita

Musa aelezea baraka kama mtu ambaye angeweza kukuwavamia kwa mshituo au nafasi na kuzishika. "Yahwe atakubariki kwa njia hizi ambazo zitakushitusha kabisa, na itakuwa kama hautakwepa yeye kukubariki"

Deuteronomy 28:3

Habari ya jumla

Musa uzungumza na Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "wako" hapa ni umoja.

Kubarikiwa itakuwa kwako

Hii inaweza kusemwa kwa mfumo kazi. "Yahwe atakubariki"

kwenye mji...kwenye shamba

Hii "merism" umaanisha kwamba Yahwe atawabariki popote.

matunda ya mwili wako, na matunda ya ardhi yako, na matunda ya wanyama

Hizi ni nahau kwa " watoto wako, na mazao yako, na wanyama wote wako" umbo la "merism" kwa kila kitu Waisraeli wathaminio.

matunda ya wanyama, ongezeko la mifugo yako, na kundi la wanyama wadogo

Kujirudiarudia mara mbili kuko katika njia tatu za kusema kwamba Yahwe atawafanya wanyama wa Waisraeli wengi na wenye nguvu. "wanyama wako wote pamoja na ndama wa ng'ombe na kundi la kondoo"

Deuteronomy 28:5

Habari ya jumla

Musa uzungumza na Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa ni umoja.

Ubarikiwa

Hii inaweza kusemwa kwa mfumo kazi. "Yahwe atakubariki"

vikapu vyako na chombo cha kukandia

Waisraeli walitumia kikapu kubeba nafaka. Chombo cha kukandia lilikuwa bakuri walilotumia kuchanganyia nafaka na kutengeneza mkate.

wakati unakuja ndani...wakati unaenda nje

"merism" urejea kwa shughuli zote za maisha kila sehemu walipoenda.

Deuteronomy 28:7

Habari ya jumla

Musa azungumza na Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa ni umoja.

kusababisha maadui zako wanaoinuka dhidi yako kupigwa chini mbele zako

Hii inaweza kusemwa kwa mfumo kazi. "kusababisha wewe kuwashinda majeshi ambayo yanawavamia"

lakini watakimbia mbele yako njia saba

"lakini watakimbia mbali kutoka kwako kwa njia saba"

njia saba

"kwa njia nyingi tofauti"

Yahwe ataamuru baraka kuja kwako katika maghala yako

Musa amwelezea Yahwe kuwabariki Waisraeli kama Yahwe alikuwa anamwamuru mtu kuwavamia kwa kumshangao.

na kwa yote ambayo unaweka mkono wako

Hii ni nahau. "na kila kitu unachofanya"

Deuteronomy 28:9

Habari ya jumla

Musa anazungumza na Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa ni umoja.

Yahwe atakuanzisha wewe kama watu ambao wametengwa kwa ajili yake

Yahwe kuchagua watu wa Israeli kuwa wake kwa njia maalumu husemwa kama Yahwe amewaweka katika eneo tofauati kutoka eneo la mataifa mengine yote yanaoishi humo. "Yahwe atakufamya wewe kuwa watu watakatifu ambao ni wake"

mnaitwa kwa jina la Yahwe

Hapa maneno "kuitwa kwa jina la Yahwe" inamaanisha kuwa wake. Hii inaweza kusemwa kwa mfumo kazi. "Yahwe amewaita wake"

Deuteronomy 28:11

Habari ya jumla

Musa anazungumza na Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa ni umoja.

matunda ya mwili wako, katika matunda ya ng'ombe zako, katika matunda ya ardhi yako

Hii ni nahau. "pmaoja na watoto, wanyama, na mazao"

ghala lake la mbinguni

Musa anazungumza juu ya mawingu ambayo mvua huanguka kama walikuwa ni jengo ambao anatunzia mvua.

kwa mkono wa kulia

"wakati mazao uhitaji"

kazi zote za mikono yako

Neno "mkono" ni neno badala la mtu mzima.

Deuteronomy 28:13

Habari ya jumla

Musa anazungumza na Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa ni umoja.

kichwa, na wala siyo mkia

Hii uelezea taifa la Israeli kama mnyama na umaanisha Waisraeli daima watakuwa viongozi juu ya mataifa mengine na kamwe watumishi watawafuata kwa nyuma. Waisraeli watakuwa bora kwa nguvu, pesa, na heshima.

watakuwa pekee juu...kamwe hawatakuwa chini

Waisraeli wataongoza wengine lakini kamwe hawatawapa wengine kuwatawala.

Ninakuamuru wewe

Musa anazungumza na Waisraeli wote, hivyo maneno "wewe" ni wingi.

kama hautageuka mbali kutoka...kwenda mkono wa kulia au kwenda wa kushoto

"kama hautatii... kwa njia yoyote"

Deuteronomy 28:15

Habari ya jumla

Musa anazungumza na Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa ni umoja

lakini kama

Hapa Musa aanza kuelezea laana watu watapata kama hawatatii.

Sauti ya Yahwe Mungu wenu

Hapa maneno "sauti ya Yahwe"umaanisha kile Yahwe asemavyo. "nini Yahwe Mungu wenu anasema"

basi laana hizi zote zitakuja kwako na kukupita

Musa aelezea laana kama mtu anavyowavamia kwa mshituko au kwa nafasi na kuwashika. "Yahwe atakulaani hivi katika njia ambazo kabisa zitakushangaza, na itakuwa kama hautatoroka akulaanipo"

Deuteronomy 28:16

Habari ya jumla

Musa anazungumza na Waisraeli kam walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa ni umoja.

Habari ya jumla

Haya maneno yalitokea mapema katika sura.

Utalaaniwa

Hii inaweza kusemwa kwa mfumo kazi. "Yahwe atakulaana wewe"

katika mji...katika shamba

Hii "merism" umaanisha kwamba Yahwe atawabariki wao kila sehemu.

kikapu chako na chombo cha kukandia

Waisraeli walitumia kikapu kubeba nafaka. "chombo cha kukandia" kilikuwa ni bakuri walilotumia kuchanganyia nafaka na kutengeneza mkate.

Deuteronomy 28:18

Habari ya jumla

Musa anazungumza na Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa ni umoja.

Habari ya jumla

Haya maneno yalitokea mapema katika sura.

Utalaaniwa

Hii inaweza kusemwa kwa mfumo kazi. "Yahwe atawalaani"

matunda ya mwili wako, matunda ya ardhi yako

Hii ni nahauu kwa ajili "watoto wako, mazao yako"

ongezeko la ng'ombe wako, na kundi la kondoo wako

Kujirudiarudia mara mbili mbili kuko kwa njia mbili kusema kwamba Yahwe atawafanya wanyama wa Waisraeli wengi na imara.

wakati unakuja ndani...wakati unaenda nje

Hii "merism" urejea kwa shughuli zote za kimaisha popote waendako.

Deuteronomy 28:20

Habari ya jumla

Musa anazungumza na Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa ni umoja

laana, machafuko, kukemea

"maafa, hofu, na kukatisha tamaa"

kwa yote unayoweka mkono wako

Hii ni nahau. "kila kitu unachofanya"

mpaka uharibiwe

Hii inaweza kusemwa kwa mfumo kazi. "mpaka maadui zako wakuharibu wewe"

kuniacha mimi

Hapa "mimi" urejea kwa Yahwe

kushikamana

kubaki kwako"

Deuteronomy 28:22

Habari ya jumla

Musa azungumza na Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa viko kwenye umoja

magonjwa ya kuambukiza, kwa homa, kwa uvimbe

Haya yote urejea kwa magonhwa ambayo husababisha watu kuwa wadhaifu na kufa. "magonjwa na kuwaka homa ambayo itawafanya kuwa dhaifu"

kwa kiangazi

"kwa upungufu wa mvua"

ukungu

ukungu ambao ukuwa kwenye mazao na kuyasababisha kuoza

Hivi vitakufukuza

Musa anazungumza kwa mambo mabaya ambayo yangeweza kutokea kwa Waisraeli kama walikuwa watu au wanyama ambayo wangewakimbiza baada ya Waisraeli.

Deuteronomy 28:23

Habari ya jumla

Musa anazungumza na Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa viko kwenye umoja.

mbingu...zitakuwa shaba

Musa anazungumza juu ya mbingu kuwa kama shaba kwa sababu hapatakuwa na mvua.

ardhi...itakuwa chuma

Musa anazungumza na ardhi kuwa kama chuma kwa sababu hakuna mazao yatakuuwa.

fanya mvua ya ardhi yako kuwa unga na vumbi

"badala ya mvua, kutakuwa na kivumbi"

hadi utakapoangamizwa

Hii inaweza kusemwa kwa mfumo kazi. "mpaka ikuangamize"

Deuteronomy 28:25

Habari ya jumla

Musa anazungumza na Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa viko kwenye umoja.

Yahwe atakusababishia upigwe mbele ya maadu zako

Hii inaweza kusemwa kwa mfumo kazi. "Yahwe atasababisha maadui zako kukupiga wewe chini"

utakimbia mbele zao kwa njia saba

Hii ina maanisha Waisraeli wataogopa na hofu na kukimbia kutoka kwa maadui zao.

njia saba

"kwa pande nyingi tofauti"

Utapelekwa huku na kule miongoni mwa falme

Hii inaweza kusemwa kwa mfumo kazi. "Watu wa mataifa mengine watawaondoa toka tafaifa moja kwa jingine"

Deuteronomy 28:27

Habari ya jumla

Musa anazungumza na Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa yako kwenye umoja

majipu ya Misri

"ugonjwa ule ule wa ngozi ambao niliwalaani Wamisri"

majipu...vidonda , kiseyeye

Haya ni aina ya magonjwa ya ngozi

ambazo hautapona

Hii inaweza kusemwa kwa mfumo kazi. "ambazo hakuna mmoja ataweza kuwaponya"

Utapapasa papasa mchana kama kipofu apapasavyo gizani

Waisraeli watakuwa na maisha magumu hata wakati kila mmoja anafurahia maisha. "watakuwa kama watu vipofu ambao upapasa gizani hata wakati wa mchana"

daima utakandamizwa na kuporwa

"watu wa nguvu sana daima watawakandamiza na kuwapora"

Deuteronomy 28:30

Habari ya jumla

Musa anazungumza na Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa yako kwenye umoja.

Ng'ombe wako atachinjwa mbele ya macho yako

Hii inaweza kusemwa kwa mfumo kazi. "Utashuhudia mtu fulani anamuawa ng'ombe wako"

punda wako atachukuliwa kwa nguvu mbele yako na hatarejeshwa kwako.

Hii inaweza kusemwa kwa mfumo kazi. "mtu fulani atamchukua punda wako kwa nguvu na hatamrudisha"

Kondoo wako watapewa maadui zako

Hii inaweza kusemwa kwa mfumo kazi. "Nitawapa kondoo zako maadui wako" au "Nitawaruhusu maadui zako kuchukua kondoo wako"

Deuteronomy 28:32

Habari ya jumla

Mus anazungumza na Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa yako kwenye umoja.

Watoto wa kiume na mabinti zako watapewa kwa watu wengine

Hii inaweza kusemwa kwa mfumo kazi. "Nitawapa watoto na binti zako kwa watu wengine" au " Maadui zako watawachukua watoto na binti zako"

macho yako yatawatafuta siku nzima, lakini yatashindwa kwa shauku juu yao.

Hapa "macho yako" urejea kwa mtu mzima. "utachoka wakati udumu kuwatazama na kutamani kuwaona tena."

Hakutakuwa na nguvu mikononi mwako.

Hapa "nguvu mkononi mwako" urejea kwa nguvu.

Deuteronomy 28:33

Habari ya jumla

Musa anazungumza na Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa yako kwenye umoja.

taifa

Hapa neno "taifa" umaanisha watu toka kwa taifa.

daima utaonewa na kugandamizwa

Maneno "kuonewa" na "kugandamizwa" kimsingi umaanisha kitu kile kile. Hii inaweza kusemwa kwa mfumo kazi. "daima wataonewa na kugandamizwa" au " watawaonea daima"

upatwe na wazimu kwa yale utakayoona yakitendeka

"kile unachoona kitakufanya kuwa wazimu"

ambayo hutaweza kupona

Hii inaweza kusemwa kwa mfumo kazi. "kwamba hakuna mmoja atakayeweza kuponya"

Deuteronomy 28:36

Habari ya jumla

Musa anazungumza na Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa yako kwenye umoja.

mithali, na uvumi, miongoni mwa watu wote ambako Yahwe atakupeleka.

Maneno "mithali" na "uvumi" kimsingi umaanisha kitu kile kile. Hii inaweza kutofasiriwa kama sentensi mpya. "na watu watafanya mithali na uvumi kuhusu wewe" au "Yahwe atakutuma wewe kwa watu ambao watakucheka wewe na kukuziaki."

uvumi

neno au kikundu cha maneno ambayo watu utumia kuwaabisha wengine.

Deuteronomy 28:38

Habari ya jumla

Musa anazungumza na Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa yako kwenye umoja/

lakini utakusanya mbegu chache

"lakini utavuna chakula kidogo sana"

Deuteronomy 28:40

Habari ya jumla

Musa aendelea kuelezea laana za Mungu kama watu hawatamtii. Anazungumza na Waisraeli kam walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa yako kwenye umoja.

lakini hautajipaka mafuta yoyote ju yako

Watu wangejipaka mafuta ya mizeituni juu yao kufanya ngozi yao kuwa na afya.

mti wako wa mzeituni utaangusha matunda yake

"mti wako wa mzeituni utaangusha matunda yake kabla hayajaiva" au "mzeituni utaanguka kwa miti ya mzeituni kabla hayajaiva"

Deuteronomy 28:42

Habari ya jumla

Musa anazungumza kwa Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa yako kwenye umoja.

atainuka juu zaidi yako juu na juu; wewe mwenyewe utashuka chini na chini.

Hii ni nahau inayomaanisha mgeni atakuwa zaidi na nguvu, pesa, na heshima kuliko Waisraeli.

atakuwa kichwa, nawe utakuwa mkia

Hii inamaanisha mgeni atakuwa kiongozi wa Waisraeli.

Deuteronomy 28:45

Habari ya jumla

Musa anazungumza kwa Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa yako kwenye umoja.

Laana hizi zote zitakujia juu yako na kukuandama na kukupita hadi utakapoangamizwa.

Musa aelezea laana kama mtu ambaye angewavamia kwa mshutuko au kuwakimbiza na kuwashika.

sauti ya Yahwe Mungu wako

Hapa maneno "sauti ya Yahwe" ni maneno kwa kile Yahwe alisema.

amri na maagizo yake

Maneno "amri" na "maagizo" ni ya kujirudiarudia mara mbili mbili kwa "yote yale Yahwe amekuamuru kufanya."

Deuteronomy 28:47

Habari ya jumla

Musa anazungumza kwa Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa yako kwenye umoja.

shangwe na furaha moyoni

Hapa "shangwe" na "furaha moyoni" umaanisha kitu kile kile. Yanasisitiza kwamba watu wanapaswa kuwa na furaha kumwabudu Yahwe.

Ataweka mzigo wa chuma juu ya shingo yako

Huu ni mfano kwa ajili ya Yahwe kumruhusu adui kuwafanyia Waisraeli kwa ukatili na kuwafanya watumwa.

Deuteronomy 28:49

Habari ya jumla

Musa anazungumza kwa Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa yapo kwenye umoja.

kutoka mwisho wa ulimwengu

Haya makundi ya maneno umaanisha kitu kile kile na kusisitiza kwamba adui atatokea taifa ambalo liko mbali sana na Israeli.

kutoka mwisho wa ulimwengu

Hii ni nahau. "kutoka maeneo ambayo haujui kitu chochote kuhusu"

kama tai arukaye kwa mhanga wake

Hii umaanisha adui atakuja kwa ghafla na Waisraeli hawataweza kuwazuia.

taifa lenye sura katili ambayo haiheshimu wazee na haionyeshi fadhila

Neno "taifa" ni mfano wa neno kwa ajili ya watu wa taifa hilo.

hadi mmeangamizwa

Hii inaweza kusemwa kwa mfumo kazi. "hadi waangamize" au " hadi wawaache bila kitu"

Deuteronomy 28:52

Habari ya jumla

Musa aendelea kueleza jeshi ambalo litawavamia Waisraeli kama hawatamtii Yahwe. Anazungumza kwa Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa yako kwenye umoja.

malango ya mji yenu

Hapa kukindi cha maneno "malango ya mji" uwakilisha mji

tunda la mwili wako mwenyewe, nyama ya watoto wa kiume na binti zako

Hapa "nyama ya watoto wako na binti zako" uelezea mfano "tunda la mwili wako mwenyewe." Watu watakuwa na njaa baada ya jeshi la maadui kuuzunguka mji wao ambao watakula watoto wao.

tunda la mwili wako mwenyewe

Hii ni nahau. "watoto wako mwenyewe"

Deuteronomy 28:54

Habari ya jumla

Musa anazungumza kwa Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa yako kwenye umoja.

ambaye ni laini na mlegevu miongoni mwenu-a

Musa anasema kwamba si wale peke yao mmoja angetegemea kula watoto wao, lakini hata mtu wa mwisho angetegemea kula watoto wake mwenyewe atakula watoto wake. "ambaye ni laini na mlegevu sana miongoni mwenu - hata yeye"

miongoni mwenu

Musa anazungumza kwa Waisraeli wote kama kundi, hivyo maneno "wewe" hapa ni uwingi.

malango yote ya mji wenu

Hapa "malango ya mji" uwakilisha miji.

Deuteronomy 28:56

Habari ya jumla

Musa anazungumza kwa Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa yako kwenye umoja.

Mwanamke laini na mlegevu miongoni mwenu...maringo

Musa anasema kwamba siyo wale peke mmoja anategemea kula watoto wao, lakini hata wanawake wa uzao wa heshima na upole wa kawaida, ambao mmoja kamwe asingetegemea kula watoto wao, watakula watoto wao. Neno "wewe" hapa ni umoja.

ambaye hatadiriki kuweka tako la mguu wake ardhini kwa sababu ya ulaini na maringo yake

Musa anatia chumvi. Anasisitiza kwamba mwanamke wa heshima yuko tajiri sana na huishi katika kifahari kwamba hataweza kujiruhusu mwenyewe kuwa mchafu.

ulaini na maringo

Hii jina "ulaini" na "maringo" yanaweza kusemwa kama kishazi

ndani ya malango ya mji wako

Hapa "malango ya mji" uwakilisha miji yenyewe.

Deuteronomy 28:58

Habari ya jumla

Musa anazungumza kwa Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa yako kwenye umoja.

ambayo yalioandikwa

Hii inaweza kusemwa kwa mfumo kazi. "ambayo nimeyaandika"

hili tukufu na la kutisha jina, Yahwe Mungu wako

Hapa "jina" urejea kwa Yahwe mwenyewe. "Yahwe Mungu wako ni wa utukufu na wa kushangaza"

Yahwe atafanya mapigo yako kuwa ya kutisha, na yale ya wazao wako;

"Yahwe atatuma mapigo ya kutisha juu yako na uzao wako" au "Yahwe atahakikisha kwamba wewe na uzao wako utateseka kwa mapigo ya kutisha"

Deuteronomy 28:60

Habari ya jumla

Musa anazungumza kwa Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa yako kwenye umoja.

Ataleta juu yako mara nyingine magonjwa yote ya Misri

"Atahakikisha kuwa tena unateseka kwa magonjwa ya Misri"

yatakung'ang'ania

magonjwa hayataacha, na hakuna mmoja ataweza kukuponya kwayo"

kila ugonjwa na pigo ambalo halijaandikwa

Huku kupigwa chuku kunaweza kusemwa kwa mfumo kazi. "hata magonjwa na mapigo ambayo sijaandika"

hadi umeangamizwa

Hii inaweza kusemwa kwa mfumo kazi. "hadi amewaangamiza"

Utabaki wachache kwa idadi... mlikuwa kama...hamkusikiliza

Musa anazungumza kwa Waisraeli kama kundi hivyo mifano yote ya "wewe" ni uwingi.

ulikuwa kama nyota wa mbinguni kwa idadi

Hii ina maanisha kwamba zamani kulikuwa na Waisraeli wengi.

sauti ya Yahwe

Hapa maneno "sauti ya Yahwe" urejea kwa kile Yahwe asemavyo.

Deuteronomy 28:63

juu yako na kutenda mema, na kuwazidisha...atafurahia juu yako kwa kufanya upotee na kwa kukuangamiza. Utang’olewa

Musa anazungumza kwa Waisraeli kama kundi, hivyo mifano yote ya "wewe" ni uwingi.

utakayoenda...atakusambaza...utaabudu...ambayo hujawajua...wewe wala mababu zako

Musa anazungumza kwa Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa yako kwenye umoja

Awali Yahwe alivyofurahia juu yako kwa kutenda mema, na kuwazidisha

"Yahwe awali alivyofurahia kutenda mema na kukusababisha wewe kuwa wengi"

atafurahia juu yako kwa kufanya upotee

"atafurahia kukufanya wewe kufa"

Utang’olewa katika nchi utakayoenda kuimiliki.

Musa anazungumza juu ya watu kama walikuwa matunda ambayo Yahwe atayaondoa kwa kichaka. Hii inaweza kusemwa kwa mfumo kazi. "Atawaondoa kutoka kwenye nchi ambayo mnaingia kuimiliki"

kutoka mwisho mmoja wa dunia hadi mwisho mwingine wa dunia;

Hizi kulikokithiri kuwili kwa pamoja umaanisha kila sehemu duniani.

Deuteronomy 28:65

Habari ya jumla

Musa anazungumza kwa Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" ma "yako" hapa yako kwenye umoja.

hakutakuwa na pumziko chini ya miguu yako

Hapa kikundi cha maneno "chini ya miguu yako" urejea kwa mtu mzima.

Yahwe atakupatia huko moyo wa kutetemeka, macho yanayofeli na nafsi inayoomboleza.

Hii ni nahau. "Yahwe atakusababisha wewe kuogopa, pasipo tumaini, na huzuni"

Maisha yako yataning'inia kwa mashaka mbele yako

"Hautajua kama utaishi au kufa"

Deuteronomy 28:67

Habari ya jumla

Musa anazungumza kwa Waisraeli kama walikuwa mtu mmoja, hivyo maneno "wewe" na "yako" hapa yako kwenye umoja.

kwa sababu ya hofu moyoni mwenu

Hii ni nahau. "kwa sababu ya hofu mliyonayo"

vitu ambavyo macho yako italazimu kuona

Hapa "macho" urejea kwa mtu mzima.

nilikuambia

Hapa "ni" urejea kwa Yahwe.

utajitoa kuuzwa kwa maadui zako...kuwanunua

Musa anazungumza kwa Waisraeli kama kundi, hivyo mifano yote ya "wewe" na "yako mwenyewe" ni uwingi.

Deuteronomy 29

Deuteronomy 29:1

Haya ni maneno ambayo Yahwe alimuamuru Musa kuwaambia

Hii ina maana ya maneno ambayo Musa anataka kuzungumza.

katika nchi ya Moabu

Hii ipo mashariki mwa upande wa Yordani ambapo Waisraeli walikuwa wakikaa kabla hawajaingia katika nchi ya Kaanani. "walipokuwa katika nchi ya Moabu"

maneno ambayo yaliongezwa katika agano ... kule Horebu

Hizi amri za ziada zilitolewa kufanya agano la Yahwe kueleweka vizuri zaidi kwa watu pale watakapokaa katika nchi yao mpya. Amri hizi mpya hazikuwa za agano jipya, lakini ongezeko kwa agano la awali.

Deuteronomy 29:2

Mmeona kila kitu ambacho Yahwe alifanya mbele ya macho yenu

Hapa "macho" yanasisitiza ya kwamba Yahwe alitarajia wao kukumbuka ya kwamba walikiona. "Mmeona yote ambayo Yahwe alifanya ili kwamba muone na kukumbuka alichofanya"

mateso makubwa ambayo macho yenu yaliona

Hapa "macho" yanasisitiza ya kwamba Yahwe alitarajia wao kukumbuka ya kwamba walikiona. "mmeona wenyewe ya kwamba watu waliteseka vibaya"

macho yako

Musa anazungumza na Waisraeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika umoja.

ishara, pamoja na ile miujiza mikubwa

Maneno "ishara" na "miujiza" yote ina maana ya mapigo ambayo Yahwe alituma juu ya Misri. "na vitu vyote vyenye uwezo ambavyo Yahwe alifanya"

Yahwe hajawapatia moyo wa kufahamu, macho ya kuona, au masikio ya kusikia

Watu wana mioyo, macho, na masikio. Lugha hii inasema ya kwamba Yahwe hajawawezesha kuelewa kile walichokiona na kusikia kutoka kwa Yahwe, na kwa nini na namna gani wanapaswa kumtii"

hajawapatia moyo wa kufahamu

Hii ni lahaja. "kuwawezesha kuelewa"

Deuteronomy 29:5

Nimewaongoza

Yahwe anazungumza na watu wa Israeli.

miaka arobaini

"miaka 40"

ndala zako ... miguuni mwenu

Musa anazungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika umoja.

kinywaji chochote chenye ulevi

Vinywaji vyenye vileo yawezekana vilivyotengenezwa kwa mazao ya kuvundikwa. havikuwa pombe iliyochujwa.

Deuteronomy 29:7

Sihoni, mfalme wa Heshboni, na Ogu, mfalme wa Bashani

Haya ni majina ya wafalme.

walikuja dhidi yetu

Hapa "yetu" ina maana ya Musa na watu wa Israeli.

shikilia maneno ya agano hili na kuyatenda

Misemo hii miwili ina maana moja na inasisitiza ya kwamba watu walipaswa kutii amri za Mungu. "tii maneno yote ya agano hili"

Deuteronomy 29:10

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

miongoni mwa kambi yenu ... mbao zenu ... maji yako

Musa anazungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika umoja.

mgeni ambaye yumo miongoni mwa kambi yenu, kutoka kwa yule anayekata mbao zenu mpaka kwa yule atekaye

Kulikuwa na wageni wengi miongoni wa Waisraeli. "wageni ambao wamo miongoni mwenu katika kambi yenu, kutoka kwao wale wanaokata mbao na wale wanaoteka maji"

Deuteronomy 29:12

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "wako" hapa ni katika umoja.

muingie katika agano la Yahwe Mungu wenu na katika kiapo ambacho Yahwe Mungu wako anafanya na wewe leo

"kukubaliana na agano na kuapa ya kwamba utatii yote ambayo Yahwe Mungu wako anaamuru"

watu kwa ajili yake

"kikundi cha watu kinachokuwa cha kwake pekee"

Deuteronomy 29:14

ninafanya

Hapa "ninafanya" ina maana ya Yahwe. "Yahwe anafanya"

aliyesimama hapa pamoja nasi

Hapa "nasi" ina maana ya Musa na watu wa Israeli.

wale ambao hawapo hapa

"vizazi vya baadaye, ambavyo havipo hapa"

tulivyoishi

"tulikuwa watumwa"

Deuteronomy 29:17

moyo wake unamuacha Yahwe Mungu wetu leo

Hapa "moyo" ina maana ya mtu mzima, na "kumuacha" ina maana ya kukoma kutii. "ambaye hamtii Yahwe Mungu wetu tena"

mzizi wowote utakaozaa nyongo na pakanga

Musa anazungumza na mtu ambaye humsifu Mungu mwingine sirini kana kwamba alikuwa mzizi, na matendo ya uovu anayofanya kutumikia mungu huyo, na ambayo anamtia moyo wengine kufanya vile. "mtu yeyote anayeabudu miungu na kusababisha wengine kutomtii Yahwe"

mtu huyo

Mtu aliyeelezwa katika mstari wa 18.

atajifariji moyoni mwake

Hii ni lahaja. "akajipongeza" au "akajitia moyo"

ingawa natembea katika ukaidi wa moyo wangu

Hii ni lahaja. "ingawa bado ninakataa kumtii Yahwe"

Hii itaangamiza ubichi pamoja na ukavu

Hapa maneno "ubichi" na "ukavu" ni sitiari ya watu watakatifu na watu waovu. Hii inaunda mkusanyiko wa maneno yenye maana mbili tofauti ya "kila mmoja". "Hii ingesababisha Yahwe kuangamiza wote watakatifu na waovu katika nchi"

ubichi ... ukavu

Vivumishi hivi vya nambari vinaweza kutafsiriwa kama nomino. Kwa sababu mara kwa mara nchi ilikuwa kavu na watu walihitaji mvua ili mazao yao yaote, maneno haya ni sitiari kwa "kuishi ... kufa" au "mema ... mabaya". "vitu vibichi ... vitu vikavu" au "watu wema .. watu wabaya"

Deuteronomy 29:20

hasira ya Yahwe na wivu wake utambanika

Kama vile moto unavyokua katika makali, kwa hiyo hasira ya Mungu na wivu unakua katika makali. "hasira ya wivu ya Yahwe utaota kama moto"

hasira ya Yahwe na wivu wake

Hapa neno "wivu" inaelezea "hasira ya Yahwe". "Hasira ya wivu wa Yahwe"

zilizoandikwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ambayo nimeandika"

laana zilizoandikwa katika kitabu hiki vitakuwa juu yake

Musa anaeleza laana kama mtu atakayemshambulia kwa mshtuko. "Yahwe atamlaani na laana zilizoandikwa ndani ya kitabu hiki kwa njia ambazo zitamshangaza kabisa". Maneno yanayofanana yanajitokeza katika 28:15.

Yahwe ataliondoa jina lake kutoka mbinguni

Hii ina maana Mungu atawaangamiza kabisa mtu na familia yake. Baadaye watu hawatamkumbuka. Msemo wa kufanana unajitokeza katika 7:23.

Deuteronomy 29:22

Kizazi kifuatacho, watoto wako watakaoinuka baada yako

Maneno "watoto wako ...baada yako" kusema nani "kizazi kifuatacho" ni kipi.

mapigo juu ya nchi hii na magonjwa ambayo Yahwe ameyafanya yawe

"jinsi Mungu alivyolaani nchi ya Kaanani na mapigo na maradhi"

watakapoona kuwa nchi yote imekuwa salfa na chumvi ichomayo

Watu waliweka salfa na chumvi juu ya ardhi kuzuia kitu kuota. "watakapoona ya kwamba Yahwe amechoma nchi kwa salfa na chumvi"

ambapo hakuna kitu kipandwacho au kuzaa matunda

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "pale ambapo hakuna mtu awezaye kupanda mbegu na mazao hayawezi kuzaa matunda"

kama anguko la Sodoma na Gomora

Nomino inayojitegemea "anguko" inaweza kuwekwa kama ibara. "kama vile Yahwe alivyowaangamiza kabisa Sodoma na Gomora"

Adma na Seboimu

Haya ni majina ya miji ambayo Yahwe aliangamiza pamoja na Sodoma na Gomora.

katika ghadhabu na hasira yake

Nomino inayojitegemea "hasira" na "ghadhabu" kimsingi ina maana ya kitu kimoja na inaweza kutafsiriwa kama msemo wa kivumishi. "alipokuwa na hasira sana"

watasema pamoja na mataifa mengine ... inamaanisha nini?

Hii inaweza kutafsiriwa kama nukuu isiyokuwa moja kwa moja. "watauliza pamoja na mataifa mengine yote kwa nini Yahwe amefanya hili juu ya nchi, na maana ya joto la hasira hii kuu ina maana gani"

watasema pamoja na mataifa mengine

"vizazi vyako na watu wa mataifa mengine yote watasema"

Joto ya hasira hii kali inamaanisha nini?

Mwandishi anawasilisha wazo moja kutumia maneno mawili. "Hasira hii mbaya ina maana gani?"

Deuteronomy 29:25

Ni kwa sababu walitelekeza agano la Yahwe, Mungu wa mababu zao

Hili ni jibu la "Kwa nini Yahwe alifanya hivi katika nchi hii?" 29:22. "Yahwe amefanya hivi katika nchi kwa sababu Waisraeli hawakufuata ahadi na sheria za agano lake"

kutumikia miungu mingine na kuzisujudu

"walitii miungu mingine na kuiabudu"

Deuteronomy 29:27

hasira ya Yahwe imewaka dhidi ya nchi hii

Musa analinganisha Yahwe kuwa na hasira na mtu anayeanzisha moto. Hii inasisitiza nguvu ya Mungu ya kuangamiza chochote kinachomkasirisha, na inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "Yahwe amekuwa na hasira sana na nchi hii"

nchi hii, ili kuleta

Hapa "nchi" ni lugha nyingine inayowakilisha watu. "watu wa nchi hii, ili kwamba kuleta juu yao"

zilizoandikwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ambayo nimeandika"

Yahwe amewang’oa kutoka nchini ... na kuwatupa

Israeli analinganishwa na mmea mbaya ambao Yahwe ameong'oa na kuutupa nje ya bustani. "Yahwe amewaondoa kutoka katika nchi yao ... na amewalazimisha wao kuondoka"

kwa hasira, kwa ghadhanu, na kwa ghadhabu kali

Maneno "hasira" na "ghadhabu" kimsingi yana maana ya kitu kimoja na yanasisitiza ukubwa mpana wa hasira ya Yahwe. "katika hasira kubwa sana" au "kwa sababu alikuwa na hasira sana"

Deuteronomy 29:29

Mambo ya siri ni ya Yahwe Mungu wetu pekee

"Baadhi ya mambo Yahwe Mungu wetu hajayafunua, na ni yeye pekee anayajua"

yaliyofichuliwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ambayo ameyafunua"

tufanye maneno yote ya sheria hii

Maneno "maneno" ni lugha nyingine kwa "amri". "tunaweza kufanya kila kitu ambacho sheria hii inatuamuru kufanya"

Deuteronomy 30

Deuteronomy 30:1

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "wako" hapa ni katika umoja.

Vitu hivi vitakavyokuja juu yako

Hapa "vitu hivi" ina maana ya baraka na laana inayoelezwa katika sura ya 28-29. Msemo "itakavyokuja juu yako" ni lahaja ambayo ina maana ya kutokea. "Vitu hivi vyote vitakavyotokea kwako"

ambazo nimeziweka mbele yako

Hii inazungumzia juu ya baraka na laana ambazo Musa aliwaambia watu kana kwamba walikuwa vyombo ambavyo aliviweka kando mbele yao. "ambayo nimekwisha kukuambia sasa hivi

utakapozirejea akilini

Hii ni lahaja. "kumbukeni"

miongoni mwa mataifa mengine

"utakapokuwa ukiishi katika mataifa mengine"

kawapeleka

"amekulazimisha kuondoka"

kutii sauti yake

Hapa "sauti" ina maana ya kile Yahwe anachosema. "tii kile anachosema"

kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote

Lahaja ya "kwa moyo .... wote" ina maana ya "yote" na "yako yot ... nafsi" ina maana "na nafsi yako yote". Misemo hii miwili ina maana moja. "kwa nafsi yako yote" au "kwa nguvu zako zote"

atageuza kutekwa kwako

"kuwaweka huru kutoka kifungoni kwako". Nomino inayojitegemea ya "kutekwa" inaweza kutafsiriwa kama kishazi. "kukuweka huru kutoka kwa yule aliyekukamata"

Deuteronomy 30:4

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika umoja.

Iwapo yeyote ya watu walio uhamishoni wapo katika sehemu za mbali sana

"Hata wale watu walio uhamishoni ambao wapo katika sehemu za mbali sana"

chini ya mbingu

"chini ya mbingu" au "juu ya dunia"

Deuteronomy 30:6

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "wako" hapa ni katika umoja.

atatahiri moyo wako

Hii sio kutoa kwa nyama kihalisia. Ina maana ya kuwa Mungu atatoa dhambi yao na kuwawezesha kumpenda na kumtii yeye.

kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote

Hii lahaja ya "kwa moyo .... wote" ina maana ya "yote" na "yako yot ... nafsi" ina maana "na nafsi yako yote". Misemo hii miwili ina maana moja. "kwa nafsi yako yote" au "kwa nguvu zako zote"

kutii sauti ya Yahwe

Hapa "sauti" ina maana ya kile Yahwe anasema. "tii kile Yahwe anasema"

ataweka laana hizi zote kwa maadui zako

Musa anazungumzia laana kana kwamba walikuwa mzigo au kifuniko ambacho mtu angeweza kuweka kihalisia juu ya mtu. "atasababisha adui zako kuteseka kutokana na laana hizi"

Deuteronomy 30:9

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika umoja.

kazi yote ya mkono wako

Hapa "mkono" ina maana ya mtu mzima. "katika kazi yako yote unayofanya"

katika matunda ya mwili wako ... katika matunda ya mifugo yako ... katika matunda ya nchi yako

Misemo hii mitatu ni lahaja ya "kwa watoto ... kwa ndama ... kwa mazao."

zilizoandikwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ambayo nimeandika"

kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote

Hii lahaja ya "kwa moyo .... wote" ina maana ya "yote" na "yako yot ... nafsi" ina maana "na nafsi yako yote". Misemo hii miwili ina maana moja. "kwa nafsi yako yote" au "kwa nguvu zako zote"

Deuteronomy 30:11

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika umoja.

wala haipo nje ya uwezo wako kufikia

Musa anazungumza kuweza kuelewa amri inahitaji mtu afanye nini kana kwamba mtu huyo anaweza kufikia kitu halisia. "wala sio vigumu sana kwako kuelewa kile Yahwe anahitaji ufanye"

Nani atayekwenda kwa ajili yetu mbinguni na kutuletea kwetu na kutufanya tuisikie, ili tuweze kuifanya?

Hapa Musa anatumia swali la balagha kusisitiza ya kwamba watu wa Israeli wanafikiri kuwa amri za Yahwe ni ngumu sana kwao kuzifahamu. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Mtu anaweza kusafiri kwenda mbinguni kujifunza amri za Mungu na kisha kurudi kutuambia walichokiona ili tuweze kukitii"

Deuteronomy 30:13

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "wako" hapa ni katika umoja.

Nani atakwenda ng’ambo ya pili ya bahari kwa ajili yetu na kutuletea kwetu na kutufanya tuisikie, ili tuweze kuifanya?

Hili swali la balagha linaendeleza wazo ya kwamba watu wa Israeli wanafikiri amri za Yahwe ni ngumu sana kufahamu. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Mtu anatakiwa kusafiri katika bahari kujifunza amri za Mungu na kisha kurudi na kutuambia zikoje"

katika kinywa chako na moyo wako

Hii ina maana watu tayari wanajua amri za Mungu na wanaweza kuzisema kwa wengine.

Deuteronomy 30:15

Taarifa ya Jumla

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika umoja.

nimeweka mbele yako

Kuweka kitu pale ambapo mtu mwingine anawez kukona ni sitiari ya kumwambia mtu jambo. "nimekuambia kuhusu"

uzima na wema, mauti na uovu

Unaweza kuweka wazi maana inayojitokeza. "ni nini kizuri na kitasababisha uishi, na nini ni kiovu na kitasababisha ufe"

na kuongezeka

"na kuwa na vizazi vingi"

Deuteronomy 30:17

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "zako" hapa ni katika umoja.

Lakini moyo wako ukigeuka ... badala yake unavutwa na kusujudia miungu mingine na kuwaabudu

Hapa "moyo" una maana ya mtu mzima. Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "ukiacha kuwa mwaminifu kwa Mungu .. na watu waishio katika nchi hiyo kukushawishi kuinama chini na kuabudu miungu mingine"

kwako leo ya kwamba ... siku zako hazitaongezeka

Musa anaongea na Waisraeli kama kundi.

siku zako hazitaongezeka

Siku kuongezeka ni sitiari ya maisha marefu. "uweze kuishi muda mrefu"

Deuteronomy 30:19

Taarifa ya Jumla:

Musa anaongea na Waisraeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, isipokuwa pale inapoandikwa neno "yako" ni katika umoja.

Naziita mbingu na nchi kushuhudia

Maana zaweza kuwa 1) Musa anawaita wale wanaoishi mbinguni na duniani kwa mashahidi kwa kile anachosema, au 2) Musa anazungumza kwa mbingu na dunia kana kwamba ni watu, na kuziita kama mahsahidi kwa kile anachosema.

kushuhudia dhidi yako

"kuwa tayari kusema ya kwamba umefanya mambo maovu"

dhidi yako leo

Musa anazungumza na Waisraeli kama kundi.

kutii sauti yake

Hapa "sauti" ina maana ya kile Yahwe alischosema. "tii kile anachosema"

na kung’ang’ania kwake

"na kumtegemea yey"

Kwa maana yeye ni uzima wako na urefu wa siku zako

"Uzima wako" na "urefu wa siku zako" ni lugha nyingine kwa yule ambaye hutoa uhai na urefu wa siku. Unaweza kuunganisha misemo hii miwili ukihitaji. "Yahwe ni yeye pekee anayeweza kukuwezesha kuishi maisha marefu"

aliapa kwa mababu zako

udondoshaji wa maneno unaweza kujazwa. "aliapa ya kwamba angewapa mababu zako"

Deuteronomy 31

Deuteronomy 31:1

umri wa miaka mia moja na ishirini

"umri wa miaka 120"

Siwezi kutoka na kuingia tena

Hapa upeo wa "kutoka" na "kuingia" inatumika pamoja kumaanisha ya kwamba Musa hawezi tena kufanya kile ambacho mwenye afya anaweza kufanya. "Siwezi kwenda sehemu zote unazohitaji kwenda, kwa hiyo siwezi kuwa kiongozi wenu tena"

Mungu wako ... mbele yako ... mbele yako ... utawanyanganya ... mbele yako

Musa anazungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" na "wako" hapa ni katika umoja.

utawanyanganya

"utachukua nchi yao"

Yoshua atakwenda kabla yako, kama Yahwe alivyonena

"Yoshua atawaongoza kupita mto, kama Yahwe alivyoahidi"

Deuteronomy 31:4

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na Waisraeli.

alivyofanya kwa Sihoni na kwa Ogu, wafalme wa Waamori

Hapa "Sihoni" na "Ogu" ina maana ya wafalme wawili wa Waamori na majeshi yao. "alifanya kwa Sihoni na Ogu, wafalme wa Waamori, na kwa majeshi wake"

Uwe hodari na mwenye ujasiri mwema

"uwe hodari na jasiri"

usiogope, na usiwaogope

"usiwaogope kabisa"

Yahwe Mungu wako ... pamoja nawe ... hatakuangusha wala kukuacha

Musa anazungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" na "wako" hapa ni katika umoja.

hatakuangusha wala kukuacha

Hii inaweza kuwekwa kama tamshi poza na kutafsiriwa kwa chanya. "siku zote atatimiza ahadi zake kwako na atakuwa pamoja nawe siku zote"

Deuteronomy 31:7

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" na "wako" hapa ni katika umoja.

machoni pa Israeli yote

Hii ina maana ya kwamba watu wote wa Israeli walikuwa pale. "katika uwepo wa Waisraeli wote"

Uwe hodari na mwenye ujasiri mwema

"uwe hodari na jasiri"

utasababisha wairithi

"utawasaidia kuchukua nchi"

Deuteronomy 31:9

kuwapatia makuhani, wana wa Walawi

"kuwapatia Walawi, ambao ni makuhani"

miaka saba

"miaka 7"

wa kudumu kwa ajili ya kufuta madeni

"kwa kufuta madeni"

Sikukuu ya Vibanda

Majina mengine ya sikukuu hii ni "Sikukuu ya Tabenakulo", "Sikukuu ya Vibanda", na "Sikukuu ya Kusanyiko". Wakati wa mavuno, wakulima hutenga makazi ya muda shambani. Sikukuu hii ilifanyika baada ya mavuno ya mwisho ya mwaka.

Yahwe Mungu wako ... utasoma

Musa anazungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" na "wako" hapa ni katika umoja.

katika kusikia kwao

"ili kwamba waweze kusikia"

Deuteronomy 31:12

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na makuhani na wazee.

mgeni wako aliye miongoni mwa malango yako

Hapa "malango ya mji" yanawakilisha wao wenyewe. Musa anazungumza na Waisraeli kana kwamba walikuwa mtu moja, kwa hiyo sehemu za "wao" hapa ni katika umoja. "mgeni wako anayeishi ndani ya miji yako"

kushika maneno yote ya sheria hii

"kutii kwa uangalifu amri zote katika sheria hii"

Deuteronomy 31:14

Tazama

"Vuta nadhari kwa kile ninachotaka kukuambia"

nguzo ya wingu

Hii ilikuwa wingu zito la moshi katika umbo la mnara uliosimama.

Deuteronomy 31:16

Tazama

"Vuta nadhari kwa kile ninachotaka kukuambia"

utalala na baba zako

Hii ni njia ya upole ya kusema "utakufa". "utakufa na kujiunga na mababu zako ambao wameshakufa kabla yako"

watainuka na kujifanya kama kahaba

Kuwa kahaba ni sitiari ya kuabudu miungu mingine tofauti na Yahwe. "kuanza kutokuwa mwaminifu kwangu"

Deuteronomy 31:17

Taarifa ya Jumla:

Yahwe anaendelea kuzungumza na Musa.

hasira yangu itawaka dhidi yao

Yahwe analinganisha hasira na mtu anayewasha moto. Hii inasisitiza nguvu ya Mungu kuangamiza chochote kinachomkasirisha. Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "Nitawasha hasira yangu dhidi yao" au "Nitakuwa na hasira na wao"

Nitaficha uso wangu kwao

Hii ni lahaja. "Sitawasaidia"

watamezwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Nitawameza" au "Nitaruhusu maadui zao kuwameza"

watamezwa

Hii ni sitiari ya "kuangamizwa kabisa".

Maafa na taabu nyingi zitawakumba

Hii inaelezea maafa na taabu kama yalikuwa binadamu. "Watapatwa na maafa na taabu nyingi"

Maafa haya hayajaja kwetu ... kati yetu?

Hii inaelezea maafa na taabu kama yalikuwa binadamu. Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Maafa haya yananiangamiza .. kati yetu."

Mungu hayupo kati yetu

"Mungu hatulindi tena" au "Mungu ametuacha peke yetu"

Deuteronomy 31:19

Taarifa ya Jumla:

Yahwe anaendlea kuzungumza na Musa kuhusu Waisraeli.

Uweke vinywani mwao

Hii ni lahaja. "Wafanye wakariri na kuimba"

nchi inayotiririka kwa maziwa na asali

Hii ni lahaja. "nchi ambayo maziwa na asali zinatiririka kwa wingi" au "nchi ambayo ni sahihi kwa mifugo na kilimo".

Deuteronomy 31:21

Maovu na taabu nyingi zitakapokuja juu ya watu hawa

Hapa maovu na taabu zinaelezwa kana kwamba ni binadamu na inweza kuwapata watu. "Watu hawa watapopitia maovu na taabu nyingi"

wimbo huu utashuhudia mbele yao kama shahidi

Hii inazungumzia juu ya wimbo kana kwamba ilikuwa shahidi wa kibinadamu akishuhudia mahakamani dhidi ya Israeli.

hautasahaulika vinywani mwa uzao wao

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "vizazi vyake havitasahau kushika kinyani mwao"

hautasahaulika vinywani mwa uzao wao

Hii inaweza kuwekwa kama chanya. "uzao wao watakumbuka kushika kinywani mwao"

hautasahaulika vinywani mwa uzao wao

Lahaja ya "kusahau kutoka kinywani mwao" ina maana ya kuacha kuzungumzia juu yake. "uzao wao wataacha kuzungumzia juu yake baina yao"

mipango wanayotengeneza

Kile ambacho watu hupanga kufanya inazungumziwa kana kwamba ilikuwa kitu halisia. "kile walichopanga kufanya"

nchi niliyowaahidi

"nchi ambayo nilikuahidi ningewapatia wao"

Deuteronomy 31:22

Uwe hodari na mwenye ujasiri mwema

"Uwe hodari na jasiri"

Deuteronomy 31:24

ushahidi dhidi yako

Musa anazungumza na Walawi kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" ni katika umoja.

Deuteronomy 31:27

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na Walawi kuhusu watu wote wa Israeli.

uasi wako na shingo yako ngumu

Musa anazungumza na Walawi kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" ni katika umoja.

shingo yako ngumu

"mkaidi"

itakuaje baada ya kifo changu?

Swali hili la balagha linasisitiza jinsi watu walivyokuwa waasi. Inaweza kutafsiriwa kama kauli. "utakuwa muasi zaidi baada ya kufa kwangu"

ili nizungumze maneno haya masikioni mwao

Hapa "masikioni mwao" ina maana ya watu wenyewe. "ili kwamba niweze kuzungumza maneno ya wimbo huu kwao"

kuziita mbingu na nchi kushuhudia dhidi yao

Maana zaweza kuwa 1) Musa anawaita wale wote wanaoishi mbinguni na duniani kushuhudia kile asemacho au 2) Musa anazungumza na mbingu na dunia kana kwamba vilikuwa binadamu, na anawaita wawe mashahidi kwa kile asemacho. Msemo kama huu unajitokeza katika 30:19

mtajiharibu kabisa

"mtafanya kile ambacho ni kibaya kabisa"

kugeuka kuiacha njia niliyowaamuru

"acha kufuata maagizo niliyokupatia"

kwa sababu mtafanya yaliyo maovu machoni pa Yahwe

Hapa "machoni pa Yahwe" ina maana "kwa maoni ya Yahwe"

kwa mikono ya kazi yenu

Hapa "mikono yako" ina maana ya watu wenyewe. "kwa sababu ya kile ulichotengeneza"

Deuteronomy 31:30

Musa alinena masikioni mwa kusanyiko lote la Israeli

Hapa "masikio" ina maana ya mtu mzima. "Musa alinena kwa watu wote wa Israeli"

alinena

Maana zaweza kuwa 1) "aliimba" au 2) "alizungumza"

maneno yote ya wimbo huu

Unaweza kuweka wazi taarifa inayoeleweka. "maneno ya wimbo ambayo Yahwe alimfundisha"

Deuteronomy 32

Deuteronomy 32:1

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza wimbo wa shairi kwa watu wa Israeli.

Tega sikio, enyi mbingu ... Acha dunia isikie

Yahwe anazungumza kwa mbingu na dunia kana kwamba zinasikiliza. Maana zaweza kuwa 1) Yahwe anazungumza na wakazi wa mbinguni na duniani au 2) Yahwe anazungumza na mbingu na dunia kana kwamba ni wanadamu.

Acha mafundisho yangu yamwagike chini kama mvua ... kama mvua tulivu juu ya majani laini

Hii ina maana Yahwe anataka watu kutaka kupokea fundisho lake lenye msaada.

udondoke

Kujitokeza kwa umande.

umande

maji yanajiunda juu ya majani na nyasi juu ya asubuhi baridi.

majani laini

"mimea mipya"

mvua tulivu

mvua nzito

Deuteronomy 32:3

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza wimbo wa shairi kwa watu wa Israeli.

nitatangaza jina la Yahwe

Hii ni lahaja. "kusema jinsi gani Yahwe ni mwema"

kumpatia ukuu Mungu wetu

"hakikisha watu wanajua ya kwamba Mungu wetu ni mkuu"

Mwamba

Hii ni jina sahihi ambalo Musa anampatia Yahwe, ambaye, kama mwamba, ni mwenye nguvu na anaweza kulinda watu wake.

kazi yake

"kila kitu afanyacho"

njia zake zote ni za haki

"anafanya kila kitu kwa njia ya haki"

Yeye ni wa haki na mwadilifu

Maneno haya mawili kimsingi yana maana moja na yanasisitiza ya kwamba Yahwe ni mwenye haki na anafanya kilicho sahihi.

Deuteronomy 32:5

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza wimbo wa shairi kwa watu wa Israeli. Musa anaendelea kutumia lugha ya kufanana kusisitiza kile anachosema.

Wamefanya yaliyo maovu dhidi yake

"alimzuia kwa kufanya kilicho kiovu" Maneno ya kufanana yanajitokeza katika 4:15.

kizazi kiovu na kilichopindika

Maneno "kiouvu" na "kilichopindika" kimsingi ina maana moja. Musa anazitumia kusisitiza jinsi kizazi kilivyokuwa kiovu. "kizazi kilicho kiovu kabisa"

Je! Unamzawadia Yahwe kwa njia hii ... watu?

Musa anatumia swali kukaripia watu. "Unatakiwa kumpatia yahwe sifastahiki ... watu"

enyi watu wapumbavu na msiojitambua

Maneno "wapumbavu" na "msiojitambua" ina maana ya kitu kimoja na inasisitiza jinsi watu walivyo wapumbavu kwa kutomtii Yahwe. "nyie watu wapumbavu kabisa"

baba yenu ... aliwaumba ... Aliwafanya na kuwaimarisha

Musa anazungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika umoja.

Je! yeye si baba yenu, yule ambaye aliwaumba?

Musa anatumia swali kukaripia watu. Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Yahwe ni baba yako na yule aliyekuomba"

Deuteronomy 32:7

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza wimbo wa shairi kwa watu wa Israeli.

Kumbukeni ... tafakari ... baba yako ... atakuonyesha ... wazee wako ... watakuambia

Musa anazungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika umoja.

Kumbukeni

Hii ni lahaja. "Kumbuka"

siku zile za zamani

"siku za zamani". Musa ana maana ya kipindi ambapo mababu wa watu wa Israeli walikuwa hai.

tafakari juu ya miaka mingi ya nyuma

Haya ni marudio ya kile ambacho Musa amemaliza kusema katika sehemu iliyopita. Musa anataka watu wa Israeli kulenga historia yao kama taifa.

atakuonyesha

"atafanya iwe wazi kwako" au "atakuwezesha kuelewa"

alipowapatia mataifa urithi wao

Hii ni lahaja. "kuweka mataifa katika sehemu ambazo wangeishi". Maneno yanayofanana, "kuwapatia kama urithi," inajitokeza katika 4:21.

na kuweka mipaka ya watu, na alipoimarisha idadi ya miungu yao

Mungu aliwapa kila kundi la watu, pamoja na miungu yao, eneo lake mwenyewe. Kwa njia hii, alipunguza ushawishi wa miungu ya kundi la watu.

Deuteronomy 32:9

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza wimbo wa shairi kwa watu wa Israeli. Anavyozungumza kwa Waisraeli, anaongea juu yao kana kwamba walikuwa mtu mwingine na kana kwamba walikuwa mtu mmoja.

Kwa maana fungu la Yahwe ni watu wake; Yakobo ni mgao wa urithi wake

Misemo hii miwili kimsingi ina maana moja na inaweza kuunganishwa. "Uzao wa Yakobo ni urithi wa Yahwe"

Alimpata ... alimkinga na kumtunza ... alimlinda

"Alimpata Yakobo ... alimkinga na kumtunza ... alimlinda" Unaweza kutafsiri hii kana kwamba Musa alikuwa akizungumza kuhusu Waisraeli kama watu wengi. "Aliwapata mababu zetu ... akawakinga na kuwatunza .. akawalinda"

jangwa kame na livumalo upepo

Hapa "livumalo" ina maana ya sauti ambayo upepo inafanya inapovuma katika nchi tupu.

alimlinda kama mboni ya jicho lake

Hii ni lahaja. Mboni ya jicho ina maana ya sehemu ya giza ya jicho ambayo humruhusu mtu kuona. Hii ni sehemu muhimu sana ya mwili. Hii ina maana ya kwamba watu wa Israeli ni muhimu sana kwa Mungu na kitu anachokilinda. "alimlinda kama kitu chenye thamani sana.

Deuteronomy 32:11

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza wimbo wa shairi kwa watu wa Israeli.

Kama tai akichungaye kiota chake na kupiga piga mabawa juu ya makinda yake, Yahwe alitandaza mabawa yake na kuwachukua, na kuwabeba kwenye mapapatio yake

Hii ina maana Yahwe aliwachunga na kuwalinda Waisraeli walipokuwa jangwani.

mapapatio

sehemu ya nje ya ukingo wa mabawa ya ndege

alimuongoza ... pamoja naye

Musa anazungumza na Waisraeli tena kama "Yakobo" (32:9). Unaweza kuhitaji kutafsiri kana kwamba Musa alikuwa akizungumza na Waisraeli kama watu wengi. "aliwaongoza .. pamoja nao"

Deuteronomy 32:13

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza wimbo wa shairi kwa watu wa Israeli.

Alimfanya aendeshe katika maeneo ya juu ya nchi

Hii ni lahaja. Neno "alimfanya" ina maana ya watu wa Israeli. "Yahwe aliwafanya waendeshe juu sehemu za juu ya nchi" au "Yahwe aliwasaidia kuchukua na kukaa juu ya nchi"

Alimfanya aendeshe ... alimlisha ... alimrutubisha

Musa anaendelea kuzungumza na Waisraeli kama "Yakobo" (32:9). Unaweza kutafsiri hiki kana kwamba Musa alikuwa akizungumzia Waisraeli kama watu wengi. "alifanya mababu zetu kuendesha ... aliwalisha .. aliwarutubisha"

alimlisha matunda ya mbugani

"alimleta katika nchi ya mazao mengi awezavyo kula"

alimrutubisha kwa asali kutoka kwenye jiwe, na mafuta kutoka kwenye mwamba mgumu sana

Nchi ilikuwa na nyuki pori nyingi, ambazo hutoa asali, pamoja na mzinga wa nyuki ndani ya mashimo ya mawe. Kulikuwa na miti mingi ya mizeituni, ambayo hutoa mafuta, na huota juu ya mawe, vilima na milima.

alimrutubisha kwa asali

Hii ni kama mama akimpatia mchanga ziwa lake. "alimruhusu kunyonya asali"

Deuteronomy 32:14

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza wimbo wa shairi kwa watu wa Israeli. Anazungumza kwa Waisraeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika umoja.

Alikula

Musa anaendelea kuzungumza na Waisraeli kama "Yakobo" (32:9). Unaweza kutafsiri hiki kana kwamba Musa alikuwa akizungumzia Waisraeli kama watu wengi. "Mababu zetu walikula"

mafuta ya wanakondoo, kondoo dume wa Bashani na mbuzi

Watu wa Israeli walikuwa na makundi mengi yenye afya ya wanyama.

Deuteronomy 32:15

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza wimbo wa shairi kwa watu wa Israeli.

Yeshuruni

Musa anazungumzia Waisraeli kana kwamba walikuwa mnyama aliyelishwa vizuri ambaye mmiliki wake alimuita Yeshuruni. Unaweza kuongeza maandishi yanayosema, "Jina la "Yeshuruni" ina maana ya "mnyoofu". Kama lugha yako haiwezi kuzungumza juu ya Waisraeli kama Yeshuruni, unaweza kuwasema Waisraeli kama watu wengi.

akakua kwa unene na kupiga mateke

Yeshuruni, mnyama aliyelishwa vizuri ambaye hupiga mateke badala ya kuwa mpole ni sitiari ya Waisraeli, ambao waliasi ingawa Mungu aliwatunza.

ulikua kwa unene, ulikua mnene sana, na ulikuwa umekula ujazo wako

Musa anawakaripia Waisraeli kwa kuzungumza ndani ya wimbo kwa Yeshuruni. "ukawa mnene, ukwa mnene zaidi, na ukawa mnene kadri uwezavyo kuwa"

Mwamba wa wokovu wake

Hii ina maana Yahwe ana nguvu kama mwamba na anaweza kuwalinda watu wake.

Mwamba

Hii ni jina stahiki ambalo Musa anampatia Yahwe, ambaye, kama mwamba, ana nguvu na anaweza kuwalinda watu wake.

Walimfanya Yahwe apatwe wivu

Waisraeli walimfanya Yahwe awe na wivu.

Deuteronomy 32:17

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza wimbo wa shairi kwa watu wa Israeli.

Walitoa sadaka

"Watu wa Israeli walitoa sadaka"

miungu ambayo imejitokeza hivi karibuni

Hii ina maana Waisraeli hivi karibuni walijua kuhusu miungu hawa.

baba zako

Musa anazungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika wingi.

Umetelekeza ... baba yako ... ukasahau ... aliyekuzaa

Musa anazungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" na "wako" hapa ni katika umoja.

Umetelekeza Mwamba

Hapa Yahwe anaitwa mwamba kwa sababu ana nguvu na analinda. "Umeacha matunzo ya kilinzi ya Yahwe"

Mwamba

Hii ni jina stahiki ambalo Musa anampatia Yahwe, ambaye, kama mwamba, ana nguvu na anaweza kuwalinda watu wake.

ambao ulikuwa baba yako ... aliyekuzaa

Hii inamlinganisha Yahwe na baba na mama. Hii ina maana ya kwamba Mungu aliwasababisha waishi kuwa taifa. "aliyekuwa baba yako ... aliyekupa uhai kwako"

Deuteronomy 32:19

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza wimbo wa shairi kwa watu wa Israeli.

wana wake wa kiume na mabinti zake

Hii ina maana ya watu wa Israeli ambaye Yahwe aliwapa uzima na kuwafanya kuwa taifa.

Nitaficha uso wangu kwao

Hii ni lahaja. "Nitageuka kutoka kwao" au "Nitaacha kuwasaidia"

nitaona mwisho wao utakuaje

"Nitaona nini kitatokea kwao"

Deuteronomy 32:21

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza wimbo wa shairi kwa watu wa Israeli. Anaendelea kutoa nukuu maneno ya Yahwe.

Wamenifanya kuwa na wivu

Hapa "wamenifanya" ina maana ya Yahwe.

kile ambacho sio mungu

"ambayo ni miungu ya uongo"

mambo yao yasiyo na maana

Unaweza kuweka wazi ambayo "vitu" ni nini. "sanamu zisizo na maana"

wale ambao sio taifa

"watu ambao hawapo miongoni mwa kundi moja la watu"

taifa pumbavu

Maneno "wapumbavu" na "msiojitambua" ina maana ya kitu kimoja na inasisitiza jinsi watu walivyo wapumbavu kwa kutomtii Yahwe. "nyie watu wapumbavu kabisa"

Deuteronomy 32:22

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza wimbo wa shairi kwa watu wa Israeli. Anaendelea kutoa nukuu maneno ya Yahwe.

Kwa maana moto kuwashwa kwa hasira yangu ... misingi ya milima

Yahwe analinganisha hasira yake na moto. Hii inasisitiza nguvu yake ya kuangamiza kile kinachomkasirisha.

moto kuwashwa kwa hasira yangu na inawaka ... inameza ... inawasha

Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "Ninaanza moto kwa sababu nimekasirika, na inachoma .. inameza ... inawasha" au "napokuwa nimekasirika, ninaangamiza adui zangu kama moto, na ninaangamiza kila kitu juu ya nchi na ndani .. ninameza ... ninawasha"

hadi chini mwa Sheoli

"hadi katika dunia ya wafu"

Deuteronomy 32:23

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza wimbo wa shairi kwa watu wa Israeli. Anaendelea kutoa nukuu maneno ya Yahwe.

Nitarundia maafa juu yao

Yahwe anazungumzia mambo mabaya ambayo yangetokea kwa Waisraeli kana kwamba ilikuwa kitu kama uchafu ambao unaweza kurundikana juu ya Waisraeli. "Nitahakikisha ya kuwa mambo mengi mabaya yanatokea kwao"

nitafyatua mishale yangu yote kwao

Hapa Yahwe analinganisha mambo mabaya ambayo atahakikisha yanatokea kwa Waisraeli kwa mtu anavyofyatua mishale kutoka kwenye upinde. "Nitafanya kila niwezalo kufanya kuwaua"

Watapotea kwa njaa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. Nomino inayojitegemea ya "njaa" inaweza kutafsiriwa kama kitenzi "kuwa na njaa". "Watakuwa wadhaifu na kufa kwa sababu wana njaa"

Wata ... njaa na kumezwa kwa joto liwakalo na uharibifu mchungu

Labda maana ya "joto liwakalo" ni 1) Waisraeli watateseka kutokana na homa au 2) hali ya hewa itakuwa na joto ajabu wakati wa kiangazi na njaa. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Wata ... njaa, na joto liwakalo na maafa mabaya yatawameza" au "Wata ... njaa, na watakufa kutokana na joto lichomalo na maafa mabaya"

nitatuma kwao meno ya wanyama wa mwituni, pamoja na sumu ya vitu vitambaao mavumbini

Meno na sumu ni lugha nyingine ya wanyama wanaotumia vitu hivi kuua. "Nitatuma wanyama pori kuwauma, na vitu vitambaacho mavumbini kuwauma na kuwatia sumu"

Deuteronomy 32:25

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza wimbo wa shairi kwa watu wa Israeli. Anaendelea kutoa nukuu maneno ya Yahwe.

Nje panga litawatwaa

Hapa "panga" inawakilisha jeshi la maadui. "Waisraeli wanapokuwa nje, jeshi la adui litawaua"

hofu kuu itafanya hivyo

Yahwe anazungumzia kuwa na hofu kana kwamba ilikuwa mtu anayekuja ndani ya nyumba na kuua wale waishio ndani yake. "utakufa kwa sababu unaogopa"

mwanamume kijana na bikra nitawaangamiza, mchanga anyonyaye, na mwanamume mwenye mvi

Misemo hii inayoelezea watu wa umri tofauti imeunganishwa kumaanisha ya kuwa kila aina ya watu watakufa.

Nilisema nita ... mbali, kwamba nita ... wanadamu

Hii inaweza kutafsiriwa kama nukuu iliyo moja kwa moja. "Nilisema, "nita .. mbali, na nita... binadamu"

nitafanya kumbukumbu yao kukoma miongoni mwa wanadamu

"Nitawafanya watu wote kusahau kuhusu wao"

Deuteronomy 32:27

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza wimbo wa shairi kwa watu wa Israeli. Anaendelea kutoa nukuu maneno ya Yahwe.

Isingekuwa kwamba naogopa uchokozi wa adui

"Niliogopa uchokozi wa adui"

uchokozi wa adui

Nomino hii inayojitegemea inaweza kutafsiriwa kama kitenzi. "ya kwamba adui angenichokoza" au "ya kwamba adui angenifanya niwe na hasira"

adui

Yahwe anazungumzia kuhusu maadui wake kana kwamba walikuwa mtu mmoja. "adui wangu" au "maadui wangu"

wangehukumu kimakosa

"hawakueleweka"

Mkono wetu umeinuliwa

Hapa "mkono" inawakilisha nguvu na uwezo wa mtu. Kuinuliwa ni lahaja ya kumshinda adui. "Tumemshinda adui kwa sababu tuna nguvu zaidi"

Deuteronomy 32:28

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza wimbo wa shairi kwa watu wa Israeli. Anaendelea kutoa nukuu maneno ya Yahwe.

Laiti wangekuwa na hekima, wangeelewa hili, na kuzingatia ujio wa hatima yao

Musa anasema jambo ambalo anatamani lilikuwa kweli, lakini anajua ya kwamba hawana hekima na hawaelewi ya kuwa kutokutii kwao kutasababisha Yahwe kuleta maafa haya juu yao.

ujio wa hatima yao

Nomino inayojitegemea ya"hatima" inaweza kutafsiriwa kama kitenzi. "kile kinachokwenda kutokea kwao"

Deuteronomy 32:30

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumzia wimbo wa shairi kwa watu wa Israeli. Anaendela kunukuu maneno ya Yahwe na kuwaambia zaidi ya yale waliyopaswa kuelewa iwapo wangekuwa na hekima (32:28).

Inawezekanaje mmoja kufukuza maelfu ... Yahwe hajawaachilia kwao?

Musa anatumia swali kukaripia watu kwa kutokuwa na hekima ya kutosha kuelewa kwa nini adui zao wanawashinda. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli.

Inawezekanaje mmoja kufukuza maelfu, na wawili kuweka makumi elfu mbioni

Unaweza kuweka wazi taarifa inayoeleweka. "Inawezekanaje askari adui mmoja kufukuza wanamume 1,000, na maaskari wawili adui kusababisha wanamume wako 10,000 kukimbia"

isipokuwa Mwamba wao hajawauza

Neno la "Mwamba" lina maana ya Yahwe amnaye ana nguvu na anaweza kulinda watu wake. "isipokuwa Yahwe, Mwamba wao, asingewapa kwao"

Mwamba wao ... Mwamba wetu

"Mwamba" ni jina stahiki ambalo Musa anamptia Yakwe, ambaye, kama mwamba, ana nguvu na anaweza kulinda watu wake.

mwamba wa maadui zetu si kama Mwamba wetu

Sanamu za maadui na miungu ya uongo havina nguvu kama za Yahwe.

kama vile maadui zetu wanavyokiri

"sio tu hatusemi hivyo, lakni adui wetu wanasema hivyo pia"

Deuteronomy 32:32

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza wimbo wa shairi kwa watu wa Israeli. Anaendelea kutoa nukuu maneno ya Yahwe.

Kwa maana mzabibu wao unatoka kwenye mzabibu wa Sodoma ... vishada vyao ni vichungu

Musa analinganisha adui ambao huabudu miungu ya uongo na watu waovu wanaoishi Sodoma na Gomora na mzabibu ambayo huzaa matunda ya sumu. Hii ina maana adui zao ni waovu na watasababisha Waisraeli kufa kama Waisraeli wataanza kutenda kama watu wanavyoishi ambao wanawazunguka.

mzabibu wao unatoka kwenye mzabibu wa Sodoma, na kwenye mashamba ya Gomorra

Mzabibu ni sitiari ya kundi la watu. Ni kana kwamba mzabibu wao ulikuwa tawi la mzabibu ambalo liliota katika shamba la Sodoma na Gomora. "wanafanya ouvu kwa njia hiyo hiyo ambayo watu walioishi Sodoma na Gomora walifanya"

vishada vyao

"vishada vyao vya mizabibu"

Deuteronomy 32:33

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza wimbo wa shairi kwa watu wa Israeli. Anaendelea kutoa nukuu maneno ya Yahwe.

Mvinyo yao ni sumu ya nyoka na sumu katili ya nyoka

Musa anaendelea kulinganisha adui wa watu wa Israeli kwa mizabibu ambayo kuzaa matunda ya sumu na divai. Hii ina maana adui wao ni waovu.

nyoka

"nyoka"

Huu mpango haujafichwa kwangu kwa siri, na kufungwa kabisa katika hazina zangu?

Swali hili linasisitiza ya kwamba mipango ya Yahwe kwa watu wa Israeli inawekwa siri kama hazina ya thamani. Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. Linaweza kuwekwa pia katika hali ya kutenda. "NInajua kile nilichopanga kufanya kwa watu wa Israeli na kwa adui zake, na nimefungia mipango hiyo kama mtu anavyofungia mali yake ya thamani"

Deuteronomy 32:35

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza wimbo wa shairi kwa watu wa Israeli. Huu ni mwisho wa nukuu ya Musa ya maneno ya Yahwe ambayo inaanza katika 32:19.

Kisasi ni changu kutoa, na fidia

Maneno "kisasi" na "fidia" kimsingi ina maana moja. "Nitakuwa na kisasi na kuadhibu adui wa Israeli"

fidia

kuadhibu au kuzawadia mtu kwa kile alichofanya

mguu wao utakapotereza

Jambo baya limefanyika kwao. "hawajiwezi"

siku ya maafa kwao

"wakati wangu kuwaangamiza"

na vitu vitakavyokuja juu yao vitaharakisha kutendeka

Yahwe anazungumzia kuhusu mambo mabaya yatakayotokea kwa adui zake kana kwamba mambo mabaya walikuwa watu wanaokimbia kwa shauku kuwaadhibu. "na nitawaadhibu haraka"

Deuteronomy 32:36

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza wimbo wa shairi kwa watu wa Israeli.

Kwa maana Yahwe atatoa haki kwa watu wake

Nomino inayojitegemea ya "haki" inaweza kutafsiriwa kama kitenzi. "Kwa Yahwe atatenda haki kwa watu wake"

atawahurumia watumishi wake

"atahisi ya kuwa anahitaji kusaidia watumishi wake"

Deuteronomy 32:37

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza wimbo wa shairi kwa watu wa Israeli.

wako wapi miungu yao, mwamba ambao wamekimbilia?

Yahwe anakaripia watu wa Israeli kwa kutafuta ulinzi kutoka kwa miungu mingine. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Tazama, miungu ambayo Waisraeli walifikiri ingewalinda haijaja kuwaokoa"

miungu iliyokula sadaka zao nene na kunywa mvinyo wa sadaka zao za kinywaji?

Hapa Yahwe anawadhihaki watu wa Israeli kwa kutoa sadaka kwa miungu mingine. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Miungu ambayo Waisraeli walitoa nyama na divai kwao hawajaja kuwasaidia"

Na wainuke na kukusaidia; na wawe ulinzi kwako.

Yahwe anasema hivi kuwadhihaki Waisraeli. Anajua kuwa miungu hawa hawawezi kuwasaidia. "Sanamu hizi hata hawawezi kusimama na kuwasaidia au kuwalinda"

Deuteronomy 32:39

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza wimbo wa shairi kwa watu wa Israeli.

mimi, hata mimi

"Mimi, mimi" au "mimi mwenyewe". Yahwe anarudia "mimi" kusisitiza ya kuwa yeye pekee ndiye Mungu.

ninainua mikono yangu mbinguni na kusema

"Ninainua mkono wangu mbinguni na kuapa" au "Nimetamka kiapo". Kwa kuinua juu mkono ni ishara ya kutoa kiapo.

Niishivyo milele

"Niishivyo milele" au "Ninaapa kwa maisha yangu ambayo hayana mwisho". Kauli hii inawahakikishia watu ya kwamba kile asemacho Mungu katika 32:41-32-42 kitatokea.

Deuteronomy 32:41

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza wimbo wa shairi kwa watu wa Israeli.

Nitakaponoa panga langu lingaaro

Hii ina maana Mungu anaandaa kuhukumu na kuadhibu adui zake. "Ninaponoa panga langu ling'aaro" au "Nitakapokuwa tayari kuhukumu adui zangu"

mkono wangu utakapoanza kuleta haki

Hapa "mkono" inawakilisha mtu mzima. "nitakapokuwa tayari kuhukumu waovu"

Deuteronomy 32:42

Taarifa ya Jumla:

Musa anazungumza wimbo wa shairi kwa watu wa Israeli.

Nitafanya mishale yangu kulewa na damu, na panga langu litameza nyama kwa damu

Yahwe anazungumzia mishale kana kwamba ni watu ambao angewapa kilevi na kuwafanya walewe, na kuhusu panga kana kwamba lilikuwa mtu ambaye alikuwa na njaa sana hadi aweze kula mnyama kabla ya kutoa damu nje. Sitiari hizi ni lugha nyingine kwa askari kutumia mishale na upanga kuwaua maadui wengi. Hii pia ni lugha nyingine ya Yahwe kuwaua adui zake vitani.

kutoka kwa vichwa vya viongozi wa adui

Maana yaweza kuwa "kutoka kwa vichwa vyenye nywele nyingi vya maadui"

Deuteronomy 32:43

Taarifa ya Jumla:

Huu ni mwisho wa wimbo wa Musa.

Furahi, enyi mataifa

Musa anaongea na watu wa mataifa yote kana kwamba walikuwa wakisikiliza.

kwa maana atalipiza kisasi damu ya watumishi wake; atalipiza kisasi juu ya maadui zake

Hapa "damu ya watumishi wake" inawakilisha maisha ya watumishi wake wasio na hatia ambao waliuawa. "kwa maana atalipiza kisasi kwa adui zake, ambao waliwaua watumishi wake"

Deuteronomy 32:44

kunena ...ananena

Maana zaweza kuwa 1) "alizungumza ... kuzungumza" au 2) "aliimba ... kuimba"

masikioni mwa watu

Hapa "masikio" yanawakilisha watu wenyewe na yanasisitiza ya kwamba Musa alitaka kuhakikisha walisikia wimbo vizuri. "kwa watu ili waweze kuwa na uhakika wa kuusikia"

Deuteronomy 32:46

Aliwaambia

"Musa alisema kwa watu wa Israeli"

Imarisheni akili yenu kwa

Hii ni lahaja. "Vuta nadhari kwa" au "Fikiri kuhusu"

nimewashuhudia kwenu

Maana zaweza kuwa 1) "nimeshuhudia kwako" ikimaanisha kwa kile Yahwe alichosema atafanya kwa Waisraeli iwapo hawatatii, au 2) "Nimekuamuru" inamaana ya kile Yahwe alichowaamuru kufanya.

watoto wenu

"watoto na uzao wenu"

hili

"sheria hii ni"

jambo dogo

Tamshi poza hizi zinaweza kuwekwa katika hali ya chanya. "jambo muhimu sana"

kwa sababu ni uzima wako

"kwa sababu utaishi kama utaitii"

utarefusha siku zako

Siku ndefu ni sitiari ya maisha marefu. "kuweza kuishi muda mrefu"

Deuteronomy 32:48

milima wa Abarimu

Hili ni jina la usawa wa mlima Moabu.

Abarimu, juu ya mlima wa Nebo

"Abarimu na kupanda juu wa mlima Nebo"

mlima wa Nebo

Hii ni sehemu ya juu kabisa katika milima ya Abarimu.

mkabala na Yeriko

"katika upande mwingine wa mto wa Yordani"

Deuteronomy 32:50

Taarifa ya Jumla:

Yahwe anamaliza kuzungumza na Musa.

utakusanywa kwa watu wako

Hii ni njia ya upole ya kusema roho ya Musa itaungana na roho za ndugu zake katika ulimwengu wa wafu. "jiunge na mababu zako ambao walikufa kabla yako"

mlima wa Hori

Hili ni jina la mlima katika mpaka wa Edomu.

Meriba

Hili ni jina la sehemu katika jangwa ambapo Musa hakumtii Mungu.

jangwa la Sini

Hili ni jina la nyika katika mpaka wa kusini wa Yuda.

Deuteronomy 33

Deuteronomy 33:1

Taarifa ya Jumla:

Musa anaanza kuwabariki makabila ya Israeli. Musa anazungumza baraka kwa njia ya shairi fupi.

Yahwe alikuja kutoka Sinai na akainuka kutoka Seiri juu yao. Alingara kutoka Mlima wa Paramu

Musa analinganisha Yahwe na kuchomoza kwa jua. "Yahwe anapokuja Sinai, aliwatazama kama jua linavyochomoza kutoka Seiri na kung'aa kutoka mlima Parani"

juu yao

"juuya watu wa Israeli"

elfu kumi ya watakatifu

"malaika 10,000"

katika mkono wake wa kuume radi zilimulika

Maana zingine zaweza kuwa 1) "katika mkono wake wa kuume kulikuwa miale ya moto" au 2) "Aliwapa sheria ya moto" au 3) "Alikuja kutoka kusini, chini ya miteremko ya mlima wake"

Deuteronomy 33:3

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kubariki kabila za Israeli, ambapo alianza kufanya katika 33:1; Musa anazungumza baraka kwa njia ya shairi fupi.

Taarifa ya Jumla:

Mistari hii ni migumu kuelewa.

watu

"watu wa Israeli"

watakatifu wake wote wapo mikononi mwako ... mguuni mwako ... maneno yako

Viwakilishi nomino "mwako" na "yako" ina maana ya Yahwe. "watakatifu wa Yahwe wote wapo mikononi mwake .. miguuni mwake ... maneno yake"

watakatifu wake wote wapo mikononi mwako

Mkononi ni lugha nyingine ya nguvu na ulinzi. "unalinda watakatifu wake wote"

urithi

"miliki" au "miliki ya thamani"

Deuteronomy 33:5

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kubariki kabila za Israeli, ambapo alianza kufanya katika 33:1; baraka ni shairi fupi.

Taarifa ya Jumla:

Mstari wa 5 ni mgumu kuelewa.

pakawa na mfalme

"Yahwe akawa mfalme"

Yeshurumu

Hili ni jina lingine la Israeli.

Ruhusu Rubeni aishi

Hii inaanza baraka za Musa kwa kabila binafsi za Israeli.

lakini wanaume wake wawe wachache

Maana zingine zaweza kuwa 1) "na wanamume wake wawe wachache" au 2) "hata kama wanamume wake ni wachache"

Deuteronomy 33:7

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kubariki kabila za Israeli, ambapo alianza kufanya katika 33:1; baraka ni shairi fupi.

sauti ya Yuda

Hapa "sauti ya Yuda" ina maana ya vilio na maombi ya watu wa Yuda. "watu wa Yuda watakapoomba kwako"

kuwa msaada

Nomino inayojitegema "msaada" inaweza kutafsiriwa kama kitenzi. "msaidie kupigana"

Deuteronomy 33:8

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kubariki kabila za Israeli, ambapo alianza kufanya katika 33:1; baraka ni shairi fupi.

Thumimu yako na Urimu yako

Haya yalikuwa mawe matakatifu ambayo kuhani wakuu alibeba kifuani kwake na kutumia mara zingine kuamua mapenzi ya Mungu. Hapa "yako" ina maana ya Yahwe.

ya mwaminifu wako

"mtakatifu wako" au "yule ambaye anatafuta kukufurahisha". Hii ina maana ya kabila la Lawi.

Masa

Jina la "Masa" lina maana ya "kujaribu".

Meriba

Jina la "Meriba" lina maana ya "bishana" au "ugomvi".

Deuteronomy 33:9

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kubariki kabila za Israeli, ambapo alianza kufanya katika 33:1; baraka ni shairi fupi. Anaendelea kufafanua kabila la Lawi, ambapo alianza kufanya katika 33:8.

kwa maana alilinda neno lako

Hapa "neno" lina maana ya amri za Yahwe. "kwa maana walitii amri zako"

alilinda ... kushika

Maneno haya yote ina maana ya kuangalia na kulinda. Mara kwa mara zilikuwa sitiari kwa "kutii", lakini hapa zinaweza kutafsiriwa kwa sababu zinamaana ya muda ambapo Walawi waliwaua watu waliokuwa wakiasi dhidi ya Yahwe.

Deuteronomy 33:10

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kubariki kabila za Israeli; baraka ni shairi fupi. Anaendelea kuelezea kabila la lawi, ambapo alianza kufanya katika 33:8.

yako ... lako ... yako ... lako

Musa anazungumza na Yahwe, kwa hiyo maneno haya yote ni katika umoja.

Deuteronomy 33:11

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kubariki kabila za Israeli; baraka ni shairi fupi. Anaendelea kuelezea kabila la Lawi, ambalo alianza kufanya katika 33:8.

kubali

"kufurahishwa na" au "kufurahia kupokea"

kazi ya mikono yake

Hapa neno "mikono" lina maana ya mtu mzima. "kazi yote ambayo anafanya"

Vunja viuno vya

Viuno vilichukuliwa kiini cha nguvu. "Kuondoa nguvu ya" au "Kuangamiza kabisa"

wanaoinuka ... wanaoinuka

Msemo huu unatumika mara mbili kama sitiari. "kuinuka kupigana ... kusababisha matatizo zaidi"

wanaoinuka dhidi

Hii ni lahaja. "kupigana dhidi"

Deuteronomy 33:12

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kubariki kabila za Israeli, baraka ni shairi fupi.

Yule anayependwa na Yahwe anaishi

Hapa Musa anamaanisha ya washiriki wa kabila la Benyamini. Hii inaweza kuwekwa kwa hali ya kutenda. "Wale ambao Yahwe anawapenda anaishi"

anaishi kwa usalama

Nomino inayojitegemea "usalama" inaweza kutafsiriwa kutumia kitenzi. "anaishi ambapo hakuna mtu wa kumdhuru"

huishi katikati ya mikono ya Yahwe

Maana zaweza kuwa 1) Yahwe hulinda kabila la Benyamini kwa nguvu yake au 2) Yahwe anaishi katika eneo la mlima wa kabila la Benyamini. Katika tafsiri zote mbili, ina maana yahwe huwatunza.

Deuteronomy 33:13

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kubariki kabila za Israeli, baraka ni shairi fupi.

Kuhusu Yusufu

Hii ina maana ya kabila la Efraimu na kabila la Manase. Kabila zote mbili zilitokana kwa Yusufu.

Nchi yake na ibarikiwe na Yahwe

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "na Yahwe abariki nchi yao"

na vitu vya thamani vya mbinguni, na umande

"kwa umande wa thamani kutoka mbinguni" au "kwa mvua ya thamani kutoka mbinguni"

umande

maji ambayo hujiunda juu ya majani na nyasi katika asubuhi za baridi.

kina kilalacho chini

Hii ina maana ya maji chini ya ardhi.

Deuteronomy 33:14

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kubariki kabila za Israeli; baraka ni shairi fupi. Anaendelea kuelezea kabila la Yusufu, ambalo alianza kufanya katika 33:13.

Nchi yake na ibarikiwe

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Na Yahwe abariki nchi yake".

na vitu vya thamani mavuno ya jua

"kwa mazao bora ambayo jua ilisababisha kuota"

na vitu vya thamani mazao ya miezi

"kwa mazao bora kabisa ambayo huota mwezi hadi mwezi"

vitu vizuri ... vitu vya thamani

Musa yawezekana anamaanisha mazao ya chakula. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "matunda bora kabisa ... matunda ya thamani"

milima ya zamani

"milima ambayo ilikuwepo zamani"

milima ya milele

"milima itakayokuwepo milele"

Deuteronomy 33:16

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kubariki kabila za Israeli; baraka ni shairi fupi. Anaendelea kuelezea kabila la Yusufu, ambalo alianza kufanya katika 33:13.

Nchi yake ibarikiwe

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Na Yahwe abariki mkono wake"

wingi wake

Nomino inayojitegemea "wingi" inaweza kutafsiriwa kama kitenzi. "kile inachotoa kwa idadi kubwa"

yule aliyekuwa kichakani

Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "Yahwe, ambaye alizungumza na Musa kutoka katika kichaka kiwakacho moto"

Baraka na ifike juu ya kichwa cha Yusufu

Sitiari hii ni ya mtu anayeweka mkono wake juu ya kichwa cha mwana na kumuomba Mungu kumbariki mwana huyo. Mtu huyo hapa ni Yahwe. "Yahwe ambariki Yusufu kama baba anavyombariki mwanawe"

ifike juu ya kichwa cha Yusufu, na juu ya kichwa cha yule

Hapa "kichwa" na "juu ya kichwa" ina maana ya mtu mzima na inalenga uzao wa Yusufu. "iwe juu ya uzao wa Yusufu"

juu ya kichwa

Maana nyingine yaweza kuwa "nyusi" au "kipaji cha uso"

Deuteronomy 33:17

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kubariki kabila za Israeli; baraka ni shairi fupi. Anaendelea kuelezea kabila la Yusufu, ambalo alianza kufanya katika 33:13.

Mzawa wa kwanza wa ng’ombe, katika utukufu wake

Ng'ombe ni sitiari ya kitu kikubwa chenye nguvu. Neno "mzawa wa kwanza" ni sitiari ya heshima. "Watu wataheshimu uzao wa Yusufu, ambao ni wengi na wenye nguvu"

pembe zake ni pembe za

Pembe ni sitiari kwa nguvu. "ana nguvu kama"

kwa hawa atawasukuma

Kusukuma kwa pembe zake ni sitiari ya nguvu. "Ana nguvu kiasi kwamba atawasukuma"

maelfu makumi ya Efraimu ... maelfu wa Manase

Hii ina maana ya kabila la Efraimu litakuwa lenye nguvu kuliko kabila la Manase. "watu wa Efraimu, ambao huhesabika mara nyingi kama 10,000 ... watu wa Manase, ambao huhesabika mara nyingi kuwa 1,000"

Deuteronomy 33:18

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kubariki kila kabila la Israeli; baraka ni shairi fupi. Anazungumza na kabila za Zabuloni na Isakari kana kwamba wao ni mtu mmoja, kwa hiyo neno "kwako" na "yako" na amri "furahi" hapa ni katika umoja.

Furahi, Zabuloni, katika kutoka kwako, na wewe, Isakari, katika mahema yako

Watu wa Zabuloni walikuwa karibu na bahari kuu. Walisafiri kwa bahari na kufanya biashara na watu wengine. Watu wa Isakari walipendelea kuishi kwa amnai na kulima ardhi na kufuga mifugo. Unaweza kufanya wazi taarifa inayoeleweka.

Huko watatoa

"Ni huko ambako watatoa"

sadaka za utakatifu

"sadaka zinazokubalika" au "sadaka zinazofaa"

Maana watanyonya wingi wa bahari, na mchanga wa ufukweni

Maana zaweza kuwa 1) watafanya biashara na watu kutoka upande wa pili wa bahari au 2) walianza kutumia mchanga kutengeneza ufinyanzi"

Maana watanyonya wingi wa bahari

Neno la Kiebrania linalotafsiriwa "kunyonya" hapa lina maana ya namna mtoto ananyonya katika ziwa la mama yake. Ina maana ya watu watapata utajiri kutokana na bahari kama mtoto anavyopata maziwa kutoka kwa mama yake"

Deuteronomy 33:20

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kubariki kabila za Israeli, baraka ni shairi fupi.

Abarikiwe yule amkuzaye Gadi

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. Maana zaweza kuwa 1) "Yahwe ambariki Gadi na kumpatia nchi kubwa kuishi ndani mwake" au 2) "Watu wanatakiwa kusema ya kwamba Yahwe ni mwema kwa sababu amempatia Gadi nchi kubwa ya kuishi"

Ataishi pale kama simba jike, naye atanyakua mkono au kichwa

Hii ina maana watu wa Gadi wana nguvu na wako salama, na watawashinda adui zao vitani"

Deuteronomy 33:21

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kubariki kabila za Israeli; baraka ni shairi fupi. Anaendelea kuelezea kabila la Gadi kama mtu mmoja, ambalo alianza kufanya katika 33:20.

fungu la kiongozi

Hii ina maana ya kipande kikubwa cha ardhi ambacho kiongozi mara nyingi alichukua.

Alikuja na vichwa vya watu

"Walikutana na viongozi wote wa Waisraeli"

Alitekeleza haki ya Yahwe na maagizo yake pamoja na Israeli

"Walitii yote ambayo Yahwe aliwaamuru Waisraeli"

Deuteronomy 33:22

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kubariki kabila za Israeli, baraka ni shairi fupi.

Dani ni mwana wa simba arukaye kutoka Bashani

Watu wa Dani wana nguvu kama mwana wa simba, na wanashambulia adui zao waishio Bashani. Unaweza kuweka taarifa inayoeleweka wazi.

Deuteronomy 33:23

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kubariki kabila za Israeli; baraka ni shairi fupi. Anazungumza na uzao wa Naftali kana kwamba wao ni mtu mmoja.

aliyeridhika na fadhila

Yahwe kufurahishwa na Naftali inazungumziwa kama "fadhila" ilikuwa chakula ambacho Naftali alikuwa hadi akawa hana njaa tena. "ambaye ana mambo yote mazuri anayotamani kwa sababu Yahwe amefurahishwa naye"

kujaa kwa baraka za Yahwe

Baraka zinazungumziwa kana kwamba zilikuwa chakula ambacho Naftali alikula mpaka hakuhitaji tena. "ambaye Yahwe alimbariki ili kwamba akawa na kila kitu anachohitaji"

miliki

Musa anazungumza kana kwamba kabila la Naftali ni mtu mmoja, kwa hiyo maneno haya ni katika umoja.

nchi iliyopo magharibi na kusini

Hii ina maana ya nchi inayozunguka ziwa la Galilaya. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi.

Deuteronomy 33:24

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kubariki kabila za Israeli, baraka ni shairi fupi.

achovye mguu wake ndani ya mafuta ya zeituni

Mafuta ya zeituni yalitumika kwa chakula na kwa ajili ya ngozi ya usoni na mikononi. Miguu ilikuwa michafu, kwa hiyo kuweka miguu katika mafuta ya zeituni ilikuwa kuharibu mafuta ya thamani. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "kuwa na mafuta mengi ya zeituni hadi anaweza kuyapoteza"

Vyuma vya mji wako ... siku zako ... usalama wako

Musa anaendelea kuzungumza na kabila la Asheri kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika umoja.

Vyuma vya mji wako na viwe chuma na shaba

Miji ilikuwa na vyuma vikubwa katika malango yao kuwaweka adui nje. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "Na uwe salama na mashambulizi ya adui zako"

Deuteronomy 33:26

Yeshurumu

Hili ni jina lingine la watu wa Israeli. Ina maana ya "mwenye haki".

anayeendesha katika mbingu ... juu ya mawingu

Hii ni picha ya Yahwe akiendesha juu ya mawingu katika mbingu kama mfalme juu ya kibandawazi katika kiwanja cha vita. "anaendesha katika mbingu kama mfalme anavyoendesha katika kiwanja cha vita ... juu ya mawingu kama mfalme juu ya kibandawazi chake"

kukusaidia

"kukusaidia". Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" hapa ni katika umoja.

Deuteronomy 33:27

Mungu wa milele ni kimbilio

Nomino inayojitegemea ya "kimbilio" ambayo ina maana ya hifadhi au sehemu salama na hatari, inaweza kuwekwa kama kitenzi. "Mungu wa milele atalinda watu wake"

chini yake kuna mikono ya milele

Maneno "mikono ya milele" ni sitiari kwa ajili ya ahadi za Yahwe kulinda watu wake milele. "atawaimarisha na kuwatunza watu wake milele"

Husukuma ... naye alisema

Musa anazungumzia muda wa baadaye kana kwamba ilikuwa muda wa nyuma kusisitiza ya kwamba kile anachosema kitakuwa kweli. ""Atasukuma nje ... atasema"

mbele yako ... Angamiza

Musa anazungumza na Waisraeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "yako" na amri "angamiza" hapa ni katika umoja.

alisema, “Angamiza!”

Kama nukuu ya moja kwa moja haitafanya vizuri katia lugha yako, unaweza kuiweka kama nukuu isiyo moja kwa moja. "atakuambia kuwangamiza!"

Deuteronomy 33:28

Israeli waliishi ...Wana wa Yakobo walikuwa salama

Maana zaweza kuwa 1) Musa anazungumzia hapo baadaye kana kwamba ilikuwa zamani kusisitiza ya kwamba alichosema kitakuwa kweli, "Israeli ataishi ... uzao wa Yakobo watakuwa salama" au 2) Musa anambariki Israeli, "Israeli aishi ... na uzao wa Yakobo uweze kuwa salama"

Wana wa Yakobo

Maana zaweza kuwa 1) nyumba ya Yakobo au 2) vizazi vya Yakobo.

mbingu na idondoshe umande

Umande inazungumziwa kama kuwa mwingi sana hadi kuwa kana kwamba ilikuwa ikinyesha. Maana zaweza kuwa 1) Musa anabariki Israeli, "na umande mwingi ufunike nchi kama mvua" au 2) Musa anasema kitakachotokea hapo baadaye, "umande mwingi utafunika nchi kama mvua"

umande

maji ambayo hujiunda juu ya majani na nyasi katika asubuhi za baridi.

Deuteronomy 33:29

Taarifa ya Jumla:

Musa anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja, kwa hiyo neno "wako" na "zako" hapa ni katika umoja.

Nani kama wewe, watu waliokombolewa na Yahwe ... utukufu?

Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. Linaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "Hakuna kundi la watu wengine kama wewe ... utukufu"

ngao ...upanga

Lugha hii ya kujumlisha inamzungumzia Yahwe kuwatetea Waisraeli kutoka kwa adui zao na kuwawezesha kushambulia adui zao.

ngao ya msaada wako

Neno "ngao" ni sitiari ya Yahwe kulinda na kuteteta Waisraeli. Nomino inayojitegemea "msaada" inaweza kutafsiriwa kama kitenzi. "yule ambaye anakulinda na kukusaidia"

upanga wa utukufu wako

Neno "upanga" ni sitiari kwa ajili ya nguvu ya kuua kwa upanga ili kushinda vita. "yule ambaye anakuwezesha kushinda vita na kuwa na utukufu"

utakanyanga sehemu zao zilizoinuka

Maana zaweza kuwa 1) Waisraeli wataangamiza sehemu ambazo watu wengine wanaabudu miungu ya uongo au 2) Waisraeli watatembea juu ya migongo ya adui zao Waisraeli watakapowashinda.

Deuteronomy 34

Deuteronomy 34:1

mlima wa Nebo

Hii ni sehemu ya juu ya mlima Pisga ambao upo sehemu ya magharibi ya usawa wa mlima wa Abarimu.

Pisga

Hili ni jina la mlima sehemu ya magharibi wa usawa wa mlima wa Abarimu.

mji wa mitende

Hili ni jina lingine la Yeriko

Deuteronomy 34:4

Beth-peori

Huu ulikuwa mji Moabu.

uitazame kwa macho yako

"jionee mwenyewe"

hadi leo hii

Hii ina maana ya muda ambao hii iliandikwa au kurekebishwa, sio kipindi cha sasa cha karne ya ishirini na moja.

Deuteronomy 34:7

miaka mia moja na ishirini ... siku thelathini

"miaka 120 .. siku 30"

macho yake hayakufifia, wala nguvu asili zake hazikupungua

Hii ina maana macho yake na mwili ulikuwa bado na nguvu na afya njema.

Deuteronomy 34:9

mwana wa Nuni

Hili ni jina la baba yake Yoshua.

Yoshua ... alikuwa amejaa na roho ya hekima

Mwandishi anazungumza kana kwamba Yoshua alikuwa chombo na roho ilikuwa kitu halisia ambacho kinaweza kuwekwa ndani ya chombo. "Yahwe alimwezesha Yoshua .. kuwa na hekima sana"

Musa alimwekea mkono juu yake

Maana kamili ya kauli inaweza kuwekwa wazi. "Musu aliweka mikono yake juu yake kumweka Yoshua kando ili Yoshua amtumikie Yahwe"

Deuteronomy 34:10

Yahwe alimjua uso kwa uso

Hii ni lahaja. Ina maana ya kwamba Yahwe na Musa walikuwa na uhusiano wa karibu sana.

mambo makubwa

"ambaye alifanya mambo yote makubwa"

Joshua 1

Joshua 1:1

Yahwe

Hili ni jina la Mungu ambalo alilidhihirisha kwa watu wake katika Agano la Kale.

Nuni

Baba yake na Yoshua

Vuka mto huu wa Yordani

''Kuvuka" ina maana ya " kwenda upande mwingine wa mto,"au kusafiri kutoka upande mmoja wa mto hadi upande wa pili."

wewe pamoja na watu hawa

Neno 'wewe' humrejelea Yoshua.

Nimewapeni ninyi

Neno "ninyi' linarejelea Yoshua na taifa la Israeli.

Nyao za miguu yenu

Ina maana ya sehemu zote ambazo Yoshua atazitembelea katika safari yake ng'ambo ya Mto Yordani.

Joshua 1:4

Maelezo ya jumla

Yahweh anaendelea kuzungumza na Yoshua

Nchi yenu

Neno 'yenu' linarejelea makabila ya Israeli na si Yoshua pekee yake.

kusimama kinyume chako

Katika mstari wa 5 maneno 'chako' na 'yako' yanamrejelea Yoshua.

Sitakupungukia wala kukuacha

Maneno 'sitakupungukia' na 'kukuacha' kimsingi yanamaanisha kitu kile kile. Yahwe aliyatumia kwa pamoja ili kukazia na kuonesha kwamba hatayafanya mambo haya. "Nitakuwa pamoja nawe siku zote."

Joshua 1:6

Maelezo ya jumla

Yahwe anampa Yoshua mfululizo wa maagizo

Uwe hodari na jasiri sana

Yahwe anamwagiza Yoshua ashinde hofu zake kwa ujasiri.

Usikengeuke upande wa kulia au wa kushoto

Maneno haya yaweza kumaanisha agizo halisi. "Ifuate sheria kwa hakika" au ''Zifuate kwa ukweli na hakika"

ili uweze kufanikiwa

"kutimiza lengo lako" au "kufikia lengo lango"

Joshua 1:8

Maelezo ya jumla

Yahweh anaendelea kuongea na Yoshua

Siku zote uuongee

Hii ina maana kwamba Yoshua alitakiwa kuongea juu kitabu cha sheria mara kwa mara. Neno 'mchana na usiku' huongeza mkazo na uzito.

Kisha utastawi na kufanikiwa

Kimsingi maneno haya mawili yanamaanisha kitu kile kile na pia yanatia mkazo juu ya kufanikiwa kwa hali kubwa.

Je si mimi niliyekuagiza?

Hii inamrejelea Yahweh akimwamuru Yoshua. "Ni mimi niliyekuagiza!"

Uwe hadori na jasiri!

Yahweh anamwagiza Yoshua.

Joshua 1:10

Nendeni katika kambi na waagizeni watu, 'andaeni... kuimilik

Nukuu ya maneno yaliyo katika funga semi yaweza kuelezwa kama "Nendeni katika kambi na uwaamuru watu waandae mahitaji kwa ajili yao. Baada ya siku tatu watavuka mto huu wa Yordani na kuingia ndani yake na kuimiliki nchi ambayo Yahweh Mungu wao anawapa ili kuimiliki.

Watu

Watu wa Israeli

katika siku tatu

Siku tatu baada ya sasa

vukeni mto huu wa Yordani

"kuvuka" ina maana ya kutoka sehemu moja kwenda sehemu nyingine ya mto.

Joshua 1:12

Maneno ya jumla

Makabila ya Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manasee yalichagua kukaa mashariki mwa Mto wa Yordani.

Warubeni

Hawa ni wazawa wa Warubeni.

Wagadi

Hawa walikuwa ni wazawa wa Gadi.

Joshua 1:14

Maelezo kwa ujumla

Yoshua anaendelea kuongea na Warubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase.

Watoto wenu

"watoto wenu wadogo"

ng'ambo ya Yordani

Inarejelea upande wa mashariki wa mto Yordani. baadaye Waisraeli wengli waliweza kuishi magharibi wa Yordani, hivyo wakaaita sehemu ya mashariki "ng'ambo ya Yordani' Lakini kwa wakati huu watu wote wakali katika upande wa mashariki mwa Yordani.

kuwapa ndugu zenu pumziko

Hii inarejelea waisraeli kuwashinda manabii wao wote wanaokaa katika nchi ya Kanaani ambao walipaswa kuwashinda.

uta........ na kuimiliki

Hii ina maana ya kuishi maisha yao kwa amani katika nchi

ng'ambo ya Yordani, mahali jua linapochomoza

Inarejelea upande wa mashariki mwa mto wa Yordani.

Joshua 1:16

Maelezo ya jumla

Waisraeli hawa walikuwa ni Warubeni, Wagadi, na nusu ya kabila la Manase ambao walimjibu Yoshua.

Yeyote anayeasi maagizo yako na kutotii maneno yako

Virai hivi vya manane kimsingi vina maana moja tu na pia vinatia mkazo kuwa aina yoyote ya uasi itaadhibiwa.

atauawa

Hii inaweza kuelezwa kwa kauli tendaji: ''Tutamwua''

Uwe hodari na jasiri tu

Mungu pamoja na Waisraeli walizingatia mambo yote kuwa ya muhimu kwa Yoshua kuendelea kama kiongozi wao.

Joshua 2

Joshua 2:1

Nuni

Huyu ni baba yake na Yoshua

Shitimu

Hili ni jina la mahali katika upande wa mashariki wa Mto wa Yordani. Ina maana ya "Miti ya Akasia."

Wapelelezi

Hawa ni watu waliotembelea nchi ili kupata taarifa juu ya jinsi ya Israeli kuitwaa.

Joshua 2:4

Maelezo ya jumla

Rahabu yule kahaba aliwahifadhi wale wapelezi wawili wa Israeli ili wasidhuriwe.

Lakini mwanamke alikuwa amewachukua na kuwaficha

Tukio hili lilifanyika kabla ya wajumbe wa wafalme hawajaongea naye.

Mwanamke

Neno hili linamrejelea Rahabu, kahaba.

Machweo

Huu ni muda ambao siku inaanza kubadilika na kuwa giza la usiku.

Joshua 2:6

Lakini alikuwa amewachukua.....darini

Haya ni maelezo ya msingi na yanaeleza jinsi alivyowaficha wanaume katika 2:4

Darini

Dari lilikuwa bapa na imara, ambalo watu waweza kutembea tembea juu yake

kitani

NI mmea ambao ulikuaukiwa na nyuzi nyuzi, ambazo zilitumika kwa kutengeneza nguo

Hivyo, watu waliwafuatilia njiani

Watu waliwafuatilia wapelelezi kwasababu ya kile ambacho Rahabu alikuwa amewaambia katika 2:4

vivuko

Hizi ni sehemu za mto ambazo hazina kina kirefu cha maji kiasi kwamba watu wanaweza kuvuka kwa kutembea kwa miguu.

Joshua 2:8

walikuwa hawajalala

Hii inarejelea kwenda kulala wakati wa usiku

Ninajua kwamba Yahweh amewapa ninyi nchi

Neno 'ninyi' linawarejelea watu wa Israeli

hofu juu yenu imetuingia

"hofu yaweza kuelezewa kwa hali tofauti." " Sisi tunawaogopeni ninyi."

watayeyuka mbele yenu

Watu wenye hofu wanalinganishwa na kuyeyuka kwa barafu na kutiririkia mbali. Maana zinazokubalika ni 1)watakuwa wadhaifu mbele za uwepo wa Waisraeli 2) watasambazwa.

Joshua 2:10

Maelezo ya jumla

Rahabu anaendelea kuongea na wapelelezi wa Kiisraeli.

Bahari ya mianzi

Hili ni jina jingine la Bahari Nyekundu

Sihoni na Ogu

Haya ni majina ya wafalme wa Waamori

mioyo yetu iliyeyuka na hapakuwa na ujasiri wowote uliosalia

Virai hivi vya maneno vina maana sawa, yameunguanishwa ili kuonesha mkazo. Maneno "mioyo yetu ikayeyuka" yanalinganisha mioyo ya watu waoga na kuyeyuka kwa barafu na kutiririka.

Joshua 2:12

Maelezo ya jumla

Rahabu anaendelea kuongea na wapelelezi wa kutoka Israeli

tafadhali mniapie ... Nipeni ishara ya uhakika

Maneno haya yanafanana kimaana kumhusu Rahabu akitafuta uhakika kutoka kwa wapelelezi.

Nimekuwa mwema kwenu

Neno 'kwenu' linarejelea wapelelezi wawili

kuhifadhi maisha...mtatuokoa katika kifo

Ni njia ya upole ya kusema "msituue sisi."

Joshua 2:14

Maelezo ya jumla

Wapelelezi wa Kiisraeli wanatoa ahadi ambayo Rahabu aliiomba

Maisha yetu kwa ajli ya maisha yenu

Hii ni njia nyingine ya kusema, " Kama tukifa, mtakufa. Kama tukiishi, nanyi mtaishi."

Joshua 2:15

Maelezo ya jumla

Wapelelezi wa Israeli wanaendelea kuongea na Rahabu.

kama hautalifanya hili

jambo hili linaelezea juu ya sharti la ahadi ambalo wapelelezi walikuwa wamelifanya kwa Rahabu. Neno 'hili' linarejelea juu ya kufunga kamba katika dirisha katika 2:18

Joshua 2:18

Sentensi kiunganishi

Wapelelezi wa Kiisraeli wanafafanua sharti walilolisema katika 2:15

Maelezo ya jumla

Wapelelezi wa Kiisraeli wanaendelea kuongea na Rahabu

Na yeyote aendaye mtaani nje ya milango ya nyumba yako

Maneno haya yanaelezea juu ya sharti kwa kuweka hali ambayo yaweza kutokea

damu yao itakuwa juu ya vichwa vyao

Hii ina maana ya "kifo chao kitakuwa kwasababu ya makosa yao wenyewe"

juu ya vichwa vyao

Neno "vichwa" linawakilisha uwajibikaji binafsi

hawatakuwa na hatia yoyote

watakuwa waadilifu wasio na kosa

kama mkono utanyoshwa juu

"kama tutasababisha madhara

Joshua 2:20

Maelezo ya jumla

Wapelelezi wa Kiisraeli wanaendelea kuonge na Rahabu juu ya ahadi zao kwake

Maelezo ya jumla

Wapelelezi walimtaka Rahabu kukaa kimya juu ya safari yao la sivyo wangekuwa huru dhidi ya kiapo cha kuilinda familia yake.

Ikiwa utaongea

kiwakilishi 'u' kinamrejelea Rahabu

Yote uliyoyasema nayatimie

Rahabu alikubaliana na matakwa ya kiapo ili kuokoa familia yake

Joshua 2:22

Maelezo ya jumla

Wapelelezi wa Israeli wanaondoka Yeriko

watu waliowafuatilia walirudi

Wale watu waliowafuatilia walirudi katika mji wa Yeriko

bila kuwaona

Hili linarejelea hao watu ambao hawakuwapata wapelelezi

Joshua 2:23

Wale watu wawili walirudi

Watu wawili walirudi katika kambi ya Waisraeli

walirudi na kuvuka mto

Haya maelezo ya maana sawa yakirejelea kurudi kule walikokuwa katika kambi ya Waisraeli

kuvuka

"kuvuka'' ina maana ya kwenda upande wa pili wa ukingo wa mto. Kusafiri kutoka upande huu hadi upande wa pili wa Yordani"

Nuni

Hili ni jina la kiume; baba yake na Yoshua

kila kitu kilichotokea kwao

"mambo yote ambayo watu walikuwa wameyapata na kuyaona."

sisi

Neno hili 'sisi' linawarejelea Waisraeli

Wenyeji wote wa nchi wanayeyuka

Watu wa nchi mbele ya Israeli ni kama kitu kinachoyeyuka katika joto.

Joshua 3

Joshua 3:1

Aliamka

Maana ya neno "alimka'' ina maana ya ''kuinuka"

Shitimu

Ni sehemu katika nchi ya Moabu, maghariibi mwa Mto Yordani mahali ambapo Waisraeli walikuwa wamepiga kambi kabla ya kuingi katika nchi ya Kanaani.

Joshua 3:2

Maafisa

Hawa ni watu walioshikilia nafasi za maamlaka na kutoa maagizo

watu

Hili ni taifa la Israeli

dhiraa elfu mbili

"dhiraa 2,000" Neno ''dhiraa'' ni kipimo ambacho ni sawa na umbali kutoka kwenye kiwiko cha mkono hadi mwisho wa vidole.

Joshua 3:5

Jitakaseni ninyi wenyewe

Maneno haya yanarejelea maandalizi maalumu ya kuwa safi kidini au kiroho mbele za Mungu.

Yahweh atafanya maajabu

Yahweh atakuwa akifanya miujiza kwa ajili ya watu wote kuona na kushuhudia

Chukueni sanduku la agano

Haya yanawarejelea walawi ambao hulichukua Sanduku la Agano kwa kusudi la kulibeba kutoka sehemu moja hadi nyingine.

Joshua 3:7

Maelezo ya jumla

Yahweh anamwambia Yoshua kile ambacho kuhani alipaswa kufanya

nitakufanya kuwa mtu mkubwa

Yahweh atamheshimu Yoshua mbele ya watu wote wa Israeli.

macho ya Waisraeli

Inawarejelea Waisraeli wote watakaoona tukio hili

ukingo wa maji ya Yordani,

Yoshua ataukaribia ukingo wa Mto wa Yordani

Joshua 3:9

Maelezo ya jumla

Yoshua anawaambia kile ambacho Yahweh alikuwa yuko karibu kufanya

atawaondosha mbele yenu

Yahweh atafukuzia mbali watu wengine walioishi katika ili watoke au wauwawe.

kuvuka

"kuvuka" ina maana ya kwenda upande mwingie wa ukingo wa mto, au '' kusafiri kutoka upande kwenda upande mwingine."

Joshua 3:12

Maelezo ya jumla

Yoshua anaendelea kuwaambia Waisraeli juu ya miujiza ambayo Yahweh ataifanya

Maelezo ya jumla

Kama vile baba wa Israeli walivyovuka katika Bahari nyekundu, watu hawa watashuhudia kuvuka Mto Yordani katika nchi kavu.

nyayo za miguu

ina maana ya sehemu za chini ya miguu yao

chemichemi

Neno hili linarejelea mwelekeo wa mtiririko wa maji ya mto Yordani kuelekea Israeli.

yatasimama katika chuguu moja

Maji yatatulia katika sehemu moja. Hayatatiririka kuelekea waliko makuhani.

Joshua 3:14

sanduku la agano

Neno ''sanduku'' hapa linarejelea sanduku ambalo lina mbao za mawe

ukingo wa maji

Inarejelea sehemu ya juu ya maji kama vile ilivyo katika ukingo wa kisima ambapo maji hutiririkia katika sehemu kavu

Yordani hujaa hadi katika kingo zake zote katika kipindi chote cha mavuno

Haya ni maelezo ya msingi na yanakazia yale ambayo Yahweh anayafanya.

Joshua 3:17

Maelezo ya jumla

Uvukaji wa kimuujiza wa Mto Yordani unaendelea

Yordani

Neno hili linarejelea sehemu ya chini udongoni ya Mto Yordani

kuvuka

Neno hili lina maana ya kwenda upande mwingine wa mto. Kusafiri kutoka upande mwingine kwenda upande wa pili.

Joshua 4

Joshua 4:1

Maelezo ya jumla

Ingawa Yahweh alikuwa anaongea moja kwa moja na Yoshua, matukio yote yalihusu Israeli.

kuvuka

Neno hili lina maana ya kwenda upande mwingine wa mto. Kusafiri kutoka upande mwingine kwenda upande wa pili

Yordani

Mto Yordani

Uwape agizo hili.........

Nukuu hii inaweza kuelezwa kwa kauli isiyo ya moja kwa moja. "Uwape agizo hili wachukue mawe kumi na mbili kutoka katikati ya mto Yordani mahali ambapo makuhani walisimama katika nchi kavu na kuyaleta na kuyaweka mahali mtakapolala usiku huu."

Joshua 4:4

Maelezo ya jumla

Yoshua anawaambia watu kumi na wawili kitu cha kufanya

katikati ya Yordani. Kila mmoja wenu achukue jiwe moja mabegani

Kila mtu kati ya watu kumi na wawili walitakiwa kuchukua mawe makubwa kutoka sehemu ya chini ya Mto Yordani na kuyabeba mpaka sehemu nyingine ili kujenga jengo la ukumbusho.

Joshua 4:6

Maelezo ya jumla

Yoshua anawaambia Waisraeli maana ya fungu la mawe kumi na mawili.

Maji ya Yordani yalitengwa mbele ya sanduku la Yahweh

Sentesi hii inaweza kuelezwa katika kauli tendaji: "Yahweh aliyatenga maji ya Yordani mbele ya sanduku la agano lake"

Maji ya Yordani

Mto Yordani

yalitengwa mbele ya sanduku la Yahweh

Mto Yordani ulizuiliwa na Mungu ili usitiririke kuelekea sanduku la Agano ambalo lilikuwa limebebwa na makuhani.

maji ya Yordani yalisimamishwa

Maji yaliyotiririka katika Mto Yordani yalikoma mbele ya sanduku ili kwamba kila mtu pamoja na agano lenyewe lisafiri katika nchi kavu.

Joshua 4:8

Maelezo ya jumla

Yoshua na Israeli wanaendelea kufanya kama Yahweh alivyowaagiza.

walichukua mawe kumi na mbili kutoka katikati ya Yordani

Hii inawarejelea watu kumi na wawili waliochukua mawe kutoka udongo ulio katikati ya Mto Yordani

Kisha Yoshua akayapanga mawe kumi na mbili katikati ya Yordani

Haya yalikuwa mawe kumi na mawili ya ziada, siyo yale mawe ambayo watu kumi na wawili waliyachukua kutoka katika undongo wa mto.

Joshua 4:10

Yordani

linarejelea Mto Yordani

Watu

Linarejelea taifa la Israeli.

Kuvuka

Hii ina maana ya kwenda upande mkabala wa ukingo wa mto. "kusafiri kutoka upande mmoja kwenda upande mwingine."

mbele za watu

Hii inarejelea kuwa mbele za watu au katika macho ya watu wote. Kila mmoja aliliona sanduku lililokuwa limebebwa na makuhani.

Joshua 4:12

Kabila la Rubeni, kabila la Gadi, na nusu ya kabila la Manase walipita kama jeshi

Hawa walikuwa ni wanajeshi wa makabila matatu ambayo yalikuwa yanatimiliza wajibu wao wa kuwaongoza Waisraeli katika vita kwa ajili ya kukaa upande wa mashariki wa Mto Yordani.

kama ambavyo wa....

Neno 'wa' linarejelea watu wa Israeli

Walimheshimu Musa

Neno hili halimaanishi to kuheshimu lakini pia kutii agizo lake na kumjali kama amiri jeshi wa jeshi lao kama walivyomfuata Musa.

Joshua 4:15

Maelezo ya jumla

Yahweh anamwambia Yoshua ili awaambie makuhani watoke katika Mto Yordani.

Joshua 4:17

Maelezo ya jumla

Mwandishi alikuwa anakiweka wazi kile kilichogawanya Mto Yordani hakikuwa cha tofauti na kile kilichogawanya Bahari Nyekundu kwa ajili ya kizazi kilichotangulia.

maji ya Yordani yalirudi katika sehemu zake na kujaa hadi katika kingo zake

Mto Yordani ulikuwa ukifurika katika kingo zake na kugharikisha eneo kabla na baada ya Israeli kuvuka katika nchi kavu.

Siku nne

Siku 4

Joshua 4:19

kukwea kutoka Yordani

Hii inarejelea kipindi ambacho Israeli ilivuka Mto Yordani katika nchi kavu.

Katika siku ya kumi ya mwezi wa kwanza

Huu ni mwezi wa kwanza wa kalenda ya Kiebrania. Siku ya kumi iko karibu na mwisho wa mwezi wa tatu wa kalenda za Kimagharibi.

Mawe kumi na mawili ambayo yalichukuliwa katika Yordani

Kila kabila lilitakiwa kuchukua jiwe moja kutoka katika Mto wa Yordani ili Yoshua aweze kutengeneza kumbukumbu ya tukio la kuvuka mto.

Joshua 4:22

Maelezo ya jumla

Yoshua anaendelea kuwakumbusha watu kusudi la kurundika mawe.

waambieni watoto wenu

Ilikuwa ni kazi ya Israeli kuwafundisha watoto wao juu ya miujiza ya Mungu ili kwamba waweze kumheshimu Yahweh milele.

mkono wa Yahweh ni nguvu

Kifungu hiki kinarejelea Nguvu ya Yahweh kuwa ni wenye nguvu. "Yahweh ni Mwenye nguvu"

Joshua 5

Joshua 5:1

mioyo yao ikayeyuka, na hapakuwa na moyo wowote ndani yao

Virai hivi viwili kimsingi vinamaaanisha kitu kimoja na kutia mkazo zaidi juu ya hofu yao.

mioyo yao ikayeyuka

Hapa "mioyo" inarejelea ujasiri wao. Walikuwa wameogopa sana kana kwamba ujasiri wao uliyeyuka kama sega la asali katika moto. "Walipoteza ujasiri wao wote."

hapakuwa na moyo wowote ndani yao

Hapa neno "moyo" linarejelea juu ya utashi wao wa kupigana. "Hawana tena hamu ya kupigana"

Joshua 5:2

Tengenezeni visu vya mawe na mara moja mwatahiri wanaume wote

Kulikuwa na watu waume zaidi ya 600,000/, hivyo na ijulikane kuwa wakati Yoshua alikua ni kiongozi wa kazi hii, watu wengi walimsaidia. Twaweza kusema pia "Yoshua na waisraeli wenyewe walijitengenezea visu vya mawe........ waliwatahiri wanaume wote.

Gibea Haaraloti

Hili ni jina la mahali/sehemu ambalo lilikuwa ni kwa ajili ya kumbukumbu ya Waisraeli kujitoa kwao mbele kwa Yahweh. Ina maana ya "kilima cha magovi"

Joshua 5:4

Maelezo ya jumla

Sababu ya kuwafanya wanaume wote watahiriwe imeelezwa

watu wa vita

Hawa ni watu amba walikuwa na umri wa kutosha kuwa wanajeshi.

Joshua 5:6

hawakuitii sauti ya Yahweh

Hapa neno "sauti" linarejelea vitu ambavyo Yahweh aliyasema. "tii mambo yale ambayo Yahweh amewaagiza"

nchi inayotiririka maziwa na asali

Mungu alizungumzia juu ya nchi ambayo ilikuwa nzuri kwa wanyama na mimea kana kwamba yalikuwa ni maziwa na asali kutoka kwa wanyama na mimea ilikuwa ikitiririka katika nchi. Pia twaweza kusema "Nchi ambayo ilikuwa ni ni nzuri kwa kufugia mifugo na kukuzia mazao."

Joshua 5:8

Siku hii nimeiondoa kwenu aibu ya Misri.

Aibu yao imeongelewa kana kwamba ni jiwe kubwa lililozuia njia yao. Hapa neno "kuiondoa'' ina maana ya "kuihamisha" Au twaweza kusema, Siku hii ya leo nimeiondoa aibu yako ya Misri

Joshua 5:10

siku ya kumi na nne ya mwezi,

Hii ni siku ya karibu na mwisho wa mwezi Marchi katika Kalenda ya Nchi za Magharibi. "Siku ya kumi na nne ya mwezi wa Kwanza"

Joshua 5:12

Mana

Mana kilikuwa ni chakula cheupe cha nafaka ambacho Mungu aliwapatia Wana wa Israeli ili wale katika kipindi cha miaka 40 walioishi jangwaani baada ya kuwa wametoka Misri.

Neno 'mana' lina maana ya ''Hiki ni nini?"

Israeli, Waisraeli, taifa la Israeli.

Istilahi hii "Israeli" ni jina ambalo Mungu alimpa Yakobo. Lina maana ya "Alishindana na Mungu."

Kanaani, Wakanaani

Kanaani alikuwa ni mtoto wa Hamu, ambaye alikuwa ni mmoja kati ya wana wa Nuhu. Wakanaani walikuwa ni uzao wa Kanaani.

Joshua 5:13

aliinua macho

Hapa, neno kuinua macho linazungumziwa kana kwamba Yoshua aliinua macho yake dhahiri katika mikono yake. Maneno haya yana maana ya "aliaangalia juu"

tazama

Neno "tazama" linalotoa tahadhari kwetu ili tuweze kuzingatia kwa namna ya kipekee kwa maelezo mapya.

alikuwa amechomoa upanga wake na ulikuwa mkononi mwake

Kiwakilishi 'a' na kimilikishi 'wake' yanmrejelea mtu yule aliyekuwa amesimama mbele ya Yoshua.

Joshua 5:14

Akajibu

Kiwakilishi 'a' kinawakilisha mtu yule ambaye Yoshua alimwona

la hasha

Hili ni neno la mwanzoni la jibu la mtu kwa swali la Yoshua. "Je uko upande wetu au wa maadui zetu?"Jibu fupi hili laweza kuelezwa kama "Siko upande wenu wala upande wa adui zenu"

Yoshua akainamisha uso wake juu ya nchi akaabudu

Hili lilikuwa ni tendo la ibada/ kuabudu

Vua viatu vyako miguuni mwako

Hili lilikuwa ni tendo la heshima na unyenyekevu

Joshua 6

Joshua 6:1

Basi

Neno hili limetumika hapa kuonesha pumziko katika masimulizi. Hapa msimlizi anatueleza kwanini malango ya Yeriko yalikuwa yamefungwa

nimeweka Yeriko katika mkono wako, mfalme wake pamoja na wanajeshi wake waliofunzwa.

Sehemu hii maneno "katika mkono wako" yana maana kwamba Yahweh alimpa Yoshua uwezo wa kuwaangamiza. Pia twaweza kusema, "Ninakupatia nguvu za kuishinda Yeriko, mfalme wake, na wanajeshi wakeo waliofundishwa."

Joshua 6:3

Sentensi kiunganishi

Mungu anaendelea kuongea na Yoshua juu ya kile ambacho watu walitakiwa kukifanya.

Ni lazima mfanye hivi kwa siku sita

"Ni lazima ufanye hivi mara moja kila siku kwa siku sita"

Makuhani saba lazima wabebe tarumbeta za pembe za kondoo waume mbele za sanduku

Makuhani saba wangetembea mbele ya makuhani wengine ambao walikuwa wanalibeba sanduku na kutembea kuuzunguka mji.

Joshua 6:5

Sentensi kiunganishi

Mungu aendelea kuongea na Yoshua juu ya kile watu walichopaswa kufanya

watapuliza pembe za kondoo waume kwa nguvu kuu,

Kiwakilishi 'wa' kinarejelea makuhani saba. "Pembe za kondoo" na "tarumbeta" ni tarumbeta za pembe za kondoo dume ambazo makuhani walikuwa wakizipuliza katika 6:3

ukuta wa mji

"Huu ulikuwa ni ukuta wa nje wa mji" au "ukuta uliouzingira mji."

Joshua 6:6

Nuni

Huyu ni baba yake na Yoshua

Lichukueni sanduku la agano

"Libebeni sanduku la agano"

Joshua 6:8

Makuhani saba walibeba tarumbeta saba za pembe za kondoo mbele ya Yahweh

Maana zinazoweza kukubalika juu ya "mbele za Yahweh ni 1)"katika utii kwa Yahweh" 2) sehemu ya mbele ya sanduku la Yahweh"

walipuliza tarumbeta

"Walizipiga tarumbeta zao sana" au "makuhani walipuliza tarumbeta za pembe za beberu"

Sanduku la Yahweh liliwafuata kwa nyuma yao

Inaweza kuelezwa dhahiri kuwa kulikuwa na watu waliobeba sanduku. au " Makuhani walikuwa wamelibeba sanduku la agano la Yahweh waliwafuata kwa nyuma yao.""

walipuliza tarumbeta zao

"Walizipiga tarumbeta zao sana" au "makuhani walipuliza tarumbeta za pembe za beberu"

Joshua 6:10

Sauti yoyote isitoke vinywani Sauti yoyote isitoke vinywani

Sauti kutoka vinywani mwao inarejelea kuongea au kupiga kelele kwao

Lakini Yoshua aliwaagiza watu

Yoshua alikuwa amewaamuru watu kabla ya kuanza kutembea kwa kuuzunguka mji.

Joshua 6:12

wakipuliza tarumbeta

Hii ina maana kwamba walizipuliza tarumbeta kiasi cha kuzifanya zitoe sauti kubwa kwa mara nyingi. Pia inaweza kumaanisha kuwa "Waliendelea kuzipiga tarumbeta zao kwa nguvu," au "Makuhani waliendelea kuzipuliza pembe za kondoo dume."

Walifanya hivi

Hii ina maana ya "Waisraeli walitembea kuizunguka Yeriko mara moja kwa kila siku."

Joshua 6:15

Watu

Neno hili linawarejelea watu wa Israeli

walipiga tarumbeta

"Waliziliza tarumbeta kwa nguvu" au "kuzipuliza tarumbeta za pembe za beberu"

amewapa ninyi

Neno"ninyi" linarejelea taifa lote la Israeli.

Joshua 6:17

Sentensi kiunganishi

Yoshua anaendelea kuongea na watu wa israeli.

Mji pamoja na vitu vyote ndani yake vitatengwa kwa Yahweh kwa ajili ya uharibifu.

Sentensi hii yaweza kuelezwa kwa kauli tendaji: "Ni lazima kuzitenga kwa Yahweh mji na kila kitu ndani yake kwa ajili ya kuharibiwa"

iweni waangalifu juu ya kuchukua vitu

Kuwa mwangalifu kunaongelewa kana kwamba wao ni walinzi wenyewe. "Iweni waangalifu msivichukue vitu"

mtaleta matatizo katika kambi

Kufanya kitu fulani kinachofanya mambo mabayaa kutokea katika mji kunasemwa kama kuleta matatizo juu yake.

Hazina ya Yahweh

Mkusanyiko wa vitu vilivyotengwa kwa ajili ya kumwabudia Yahweh.

Joshua 6:20

watu wakapiga kelele

"Watu wa Israeli wapiga kelele"

Ilikuwa

Neno hili limetumika hapa kuonesha tukio muhimu katika habari.

makali ya upanga

Ingawa watu wengi wa Israeli hutumia upanga, katika sehemu hiii inarejelea mashambulizi yenye vurugu au vita kwa ujumla. Au twaweza kusema "Kwa panga zao zenye makali" au "katika vita"

Joshua 6:23

Na wakachoma mji

kiwakilishi 'wa'kinawarejelea wanajeshi wa Kiisraeli. Hairejelei wale vijana wawili tu waliowatoa nje Rahabu na familia yake.

Joshua 6:25

anaishi Israeli

Kiwakilishi 'a'kinamrejelea Rahabu na kinawakilisha uzao wake. Yaani "Uzao wake unaishi Israeli."

mpaka leo

"sasa" au "hata leo" uzao wa Rahabu ulikuwa bado unaishi Israeli wakati mwandishi wa awali alipokuwa akiandika habari hii.

Joshua 6:26

Alaaniwe machoni pa Yahweh mtu yule anayeujenga mji huu

kulaaniwa mbele la Yahweh ina maana ya kulaaaniwa na Yahweh. Yaani "Yahweh na amlaani mtu yule atakayejenga.."

Ataujenga msingi kwa gharama ya mzaliwa wake wa kwanza

Matokeo ya mtu kuweka malango mapya kwa mji wa Yeriko ilikuwa ni kwamba mwana wake wa kwanza wa kiume angekufa. Hii inaongelewa kana kwamba ilikuwa ni gharama ambayo mtu alitakiwa kuilipa. "Kama utauweka msingi, atampoteza mwana wake wa kwanza.

kwa gharama ya mzaliwa wake wa pili atapachika milango yake

Matokeo ya mtu kuweka malango mapya kwa mji wa Yeriko ilikuwa ni kwamba mtoto wake mdogo wa kiume angekufa. Hii inaongelewa kana kwamba ilikuwa ni gharama ambayo mtu alitakiwa kuilipa. "Kama utauweka msingi, atampoteza mwana wwake mdogo."

umaarufu wake ulienea

"Umaarufu wa Yoshua ulienea" Kujulikana miongoni wa watu katika nchi yote, kunasemwa kama kuenea kwa umaarufu wake. "Yoshua alijulikana na kuwa maarufu katika nchi yote.

Joshua 7

Joshua 7:1

vitu vilivyotengwa kwa ajili ya uharibifu

"Vitu ambavyo Mungu alikuwa amevisema lazima vitengwe kwa ajili yake kwa kuviteketeza"

Akani...Karmi... Zabdi...

Haya ni majina ya wanaume.

Hasira ya Yahweh ikawaka

"Hasira" na "kuwaka" yanaonesha uzito, siyo kwamba moto ulikuwapo dhahiri. "Hasira ya Yahweh iliwaka kama moto"

Joshua 7:2

Watu wote

Inarejelea jeshi lote la Israeli.

watu ni wachache

linarejelea watu wa Ai

Joshua 7:4

watu wapatao elfu tatu tu kutoka katika jeshi

Hawa ni wanaume walikuwa sehemu ya jeshi. "Watu elfu tatu waliokuwa ni sehemu ya jeshi waliopanda."

watu elfu tatu.... watu thelathini na sita

wanaume sita..-"3,000 watu ... 36 wanaume"

mioyo ya watu iliogopa... ujasiri wao uliwatoka

Vifungu hivi viwili vya maneno vina maana sawa na vimeunganishwa ili kutilia mkazo kwamba watu waliogopa sana.

mioyo ya watu

Kirai hiki kinawarejelea wanajeshi wa Kiisraeli

ujasiri wao ukawatoka

"hawakuwa na ujasiri tena ndani yao"

Joshua 7:6

alizirarua nguo zake. Yeye pamoja na wazewe wa Israeli waliweka mavumbi juu ya vichwa vyao na wakainamisha vichwa vyao hadi katika nchi mbele ya sanduku la Yahweh

Walifanya vitu hivi ili kumwonesha Mungu jinsi walivyo na huzunisshwa na kufedheheshwa.

Kutuweka katika mikono ya Waamori ili kutuangamiza?

Yoshua alikuwa anauliza kama hii ni sababu ya Mungu kuwaleta ng'ambo ya Yordani. "Je ulifanya hivi ili kututia katika mikono ya Waamori ili kututeketeza?"

Kutuweka katika mikono ya Waamori ili kutuangamiza?

Katika mikono ya Waamori inawakilisha utawala na mamlaka. Kuwatia Waisraeli katika mikono ya Waamori ni kuwaruhusu Waamori kuwa na mamlaka juu ya Waisraeli na kuwaangamiza.

ikiwa kama tulifanya maamuzi tofauti

Neno "ikiwa kama" linaonesha kuwa haya ni matakwa ambayo bado hayajatokea. "Ninatamani tungefanya maamuzi tofauti."

Joshua 7:8

Maelezo ya jumla

Yoshua anamwelezea Mungu juu ya wasiwasi uliokuwepo

niseme nini, baada ya Israeli kuwatega migongo maadui zao!

Yoshua aliyasema haya kuonesha jinsi alivyokuwa amekatishwa tamaa kana kwamba alikuwa hana hata neno la kusema. "Sijui kitu cha kusema.Israeli imegeuka na kukimbia mbele za adui zao."

Israeli kuwatega migongo maadui zao

Kufanya hivyo kunamaanisha kukimbia kutoka kwa maadui zao. "Israeli imekimbia kutoka kwa maadui zao."

watatuzunguka na kuwafanya watu wa nchi kulisahau jina letu

Kuwafanya watu wasahau jina la Israeli ina maana ya kuwafanya waasahau Waisraeli. Kwa namna hii watalifanya hili kwa kuwaua Waisraeli. "Watatuzunguka na kutuua, na watu wa dunia watatusahau sisi."

Na utafanya nini kwa ajili ya jina lako kuu?

Kifungu cha maneno "jina lako kuu" mahali hapa kina maana ya Sifa za Mungu na uweza. "Na je utafanya nini ili watu wajue kuwa wewe ni mkuu."

Na utafanya nini kwa ajili ya jina lako kuu?

Yoshua alitumia swali hili kwa ajili ya kumtahadharisha Mungu kwamba kama Waisraeli watauwawa, ndipo watu wengine watadhani kuwa Mungu si mkuu. "Hakutakuwa na kitu utakachokifanya kwa ajili ya jina lako kuu" au "Watu hawatajua kwamba wewe ni mkuu."

Joshua 7:10

Maelezo ya jumla

Yahweh anamwambia Yoshua kwanini Israeli imelaaniwa.

kwanini umelala kifudifudi?

Mungu alitumia swali hili kumkemea Yoshua kwa kulala kifudifudi. "Acha kulala hapo kifudifudi katika uchafu!."

vitu vilivyokuwa vimetengwa

Hivi ni vitu "viliwekwa kwa ajili ya kuharibiwa" kutoka katika 6:17 "Vitu vilivyolaaniwa" au "Vitu vile ambavyo Mungu amevilaani"

Wameiba na kisha pia wakaficha dhambi yao

Kuficha dhambi ina maana ya kujaribu kuwafanya watu wengine wasijue kuwa wametenda dhambi. "Wameviiba vitu vile na kisha walijaribu kuwaficha watu wasijue kuwa wametenda dhambi"

hawataweza kusimama mbele za maadui zao

Kusimama mbele ya maadui zao kuna maana ya kupigana kwa mafanikio dhidi ya maadui zao. Hivyo ina maana ya "hawataweza kupigana kwa mafanikio dhidi ya maadui zao" au "hawataweza kuwashinda maadui zao."

Walitega migongo yao kwa maadui zao

Kutega migongo kuna maana ya kukimbia mbali kutoka kwa maadui zao.

Sitakuwa pamoja nanyi tena

Kuwa pamoja na Israeli kuna maana ya kuwasaidia Waisraeli. "Sitawasaidieni tena."

Joshua 7:13

Sentensi kiunganishi

Yahweh anaendelea kuongea na Yoshua na kumwambia kitu cha kuwaambia watu

Watu

Inarejelea watu wa Israeli

Hamtaweza kusimama mbele ya maadui zenu

Kusimama mbele za maadui zao kuna maana ya kupigana kwa mafanikio dhidi yao. "Hamtaweza kuwashinda maadui zenu"

Joshua 7:14

Sentensi kiunganishi

Yahweh anaendelea kumwambia Yoshua kile anachopaswa kuwaambia watu.

mtajisogeza wenyewe kwa makabila

Kulikuwa na makabila kumi na mawili yaliyowafanya watu wa Israeli. Kifungu cha maneno "kwa makabila" kina maana ya "kila kabila"

Kabila lile ambalo Yahweh atalichagua litasogea karibu kwa koo zake

Kabila hujengwa na makabila mengi. "Kutoka katika kabila ambalo Yahweh amelichagua, kila kabila litakaribia,"

Kabila ambalo Yahweh atalichagua

Viongozi wa Israeli watapiga kura, na kwa kufanya hivi, wangejifunza ni kabila gani Yahweh alikuwa amelichagua.

Ukoo ule ambao Yahweh atauchagua lazima usogee karibu kwa nyumba

Ukoo ulijengwa na familia/nyumba kadhaa. "Kutoka katika ukoo ambao Yahweh ameuchagua, kila nyumba itasogea karibu."

Nyumba ambayo Yahweh ataichagua lazima isogee karibu kwa mtu mmoja mmoja

Nyumba iliundwa na watu kadhaa. "Kutoka katika nyumba ambayo Yahweh ameichagua, kila mtu atasogea karibu"

Itakuwa hivi mtu yule atakayechaguliwa

Maneno haya yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji "Yeye ambaye Yahweh anamchagua"

amelivunja agano la Yahweh

Kuvunja agana kuna maana ya kutolitii. "Ameliasia agano la Yahweh"

Joshua 7:16

Maelezo ya jumla

Yoshua anafuata agizo la Yahweh la kuwaleta Waisraeli mbele za Yahweh.

aliwaleta Israeli karibu

Maneno "kabila kwa kabila" lina maana ya kila kabila.

Kabila la Yuda lilichaguliwa

Maneno haya yanaweza kuelezwa kawa muundo tendaji. "Yahweh alilichagua kabila la Yuda"

Akausogeza karibu ukoo wa Zera mtu kwa mtu,

kirai "mtu kwa mtu" ina maana ya kila mtu. Watu katika sentensi hii walikuwa ni viongozi wa nyumba zao.

ukoo wa Zera

Ukoo uliitwa kawa jina la mtu aliyeitwa Zera

Zabdi...Akani...Karmi...Zera

Haya ni majina ya wanaume.

Joshua 7:19

ufanye ukiri wako kwake

Maneno "fanya ukiri wako" yaweza kufafanuliwa kwa kitenzi 'kiri' "Kiri kwake"

Usinifiche

Kuficha maelezo ina maana ya kujaribu kumficha mtu asijue. "usinizuie kujua kile ulichokifanya."

Shekeli mia mbili

Hii ni zaidi ya kilogramu mbili

shekeli hamsini

Hii ni zaidi ya gramu 500

Vimefichwa chini ardhini

Maneno haya yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Nilivificha chini ardhini."

Joshua 7:22

Walipoangalia

"Watu wale Yoshua aliwatuma waliaangalia"

Walivimwaga

kumwaga vitu vingi chini

Joshua 7:24

bonde la Akori

Jina la maana ya "bonde la matatizo," lakini ni vizuri kulitafsiri jina Akori kama linavyosikika.

Joshua 7:25

"Kwanini umetusumbua?

Yoshua anatumia swali hili kumkemea Akani. "Umetutesa"

Na wakawachoma wote kwa moto, na wakawapiga mawe

Maana zinazokubalika 1) Waisraeli waliichoma familia ya Akani hadi kifo na kisha wakawafunika kwa mawe. 2) Waisraeli waliipiga kwa mawe familia ya Akani na kisha wakaichoma kwa moto miili yao.

Yahweh akaachilia mbali hasira yake

Kuachilia mbali hasira ina maana ya kuacha kuwa na hasira. Kuwaka kwa hasira ina maana ya kuwa na hasira kali.

hata leo

Ilikuwa bado linaitwa bonde la Akori katika kipindi ambacho mwandishi aliandika. "hata leo" au "hata sasa"

Joshua 8

Joshua 8:1

Usiogope; usivunjike moyo

Vifungu hivi viwili vya maneno kimsingi vinamaanisha kitu kimoja. Yahweh ameviunganisha pamoja kutia mkazo kwamba hakuna sababu ya kuogopa.

nimemtia mkononi mwako mfalme wa Ai... na nchi yake

Kuwatia katika mkono wa Israeli ina maana ya kuwapa waisraeli ushindi na kuwatawala. "Nimewapeni ushindi dhidi ya mfalme wa Ai na watu wake, na nimewapeni utawala juu ya mji wake na nchi yake."

Nimewapeni

Mungu anaongelea juu ya ahadi alizoahidi kufanya kana kwamba alikuwa ameshakifanya, kwasababu atalifanya kwa uhakika. "NItawapa kwa uhakika"

mfalme wake

Neno 'wake' inarejelea mji wa Ai.

Joshua 8:3

watu wa vita

"jeshi la Israeli"

watu elfu thelathini

wanaume 30,000

Joshua 8:5

Maelezo ya jumla

Yoshua anaendelea to kuelezea mapango wa vita kwa wanajeshi wake

atawapa mkononi mwenu.

"mkono" inaashiria utawala na nguvu za watu walizo nazo juu ya maadui zao.

Joshua 8:8

Maelezo ya jumla

Yoshu anamalizia kueleza mpango wa vita kwa wanajeshi wake.

Yoshua akawatuma

Maneno haya yanamrejelea Yoshua akiwatuma watu thelathini walikuwa wamechaguliwa ili kuivamia Ai mahali ambapo watakaa ili kuvizia.

sehemu ya kuvizia

"mahali ambapo wangejificha mpaka wakati wa kushambulia."

Joshua 8:10

watu elfu tano

"Wanaume 5,000" Kundi hii linaonekana kuwa sehemu ya watu "elfu thelathini (8:8). Hili ni kundi dogo lilosalia katika hali ya kuvizia wakati watu wengine 25,000 walipouvamia mji.

Joshua 8:13

Maelezo ya jumla

Waisraeli wanajianda kupigana na watu wa Ai.

jeshi kubwa

kundi kubwa la watu wapiganaji, si kundi lile lililokuwa katika hali ya kusubiri

walinzi wa nyuma

wale walikuwa wamewekwa katika hali ya kuvizia upande wa magharibi mwa mji.

Joshua 8:15

walikubali wenyewe kushindwa mbele yenu

"waache washindwe mbele ya watu wa Ai." Maneno"mbele yao" yana maana ya kile ambacho watu wa Ai wakiona na kukifikiria.

walikubali wenyewe kushindwa mbele yenu

Neno "kushindwa" laweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "waache watu wa Ai wafikiri kwamba wameshawashinda Waisraeli."

mbele yao...waliwafuata...walivutwa mpaka mbali

Maneno "yao" na "wa" yanarejelea jeshi la Ai.

walikimbia... waliwafuata

Maneno haya yanalihusu jeshi la Israeli.

Watu wote waliokuwa kwenye mji waliitwa kwa pamoja

Maneno haya yanaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. " viongozi wa mji walliwaita watu wote kwa pamoja katika mji.

Watu wote waliokuwa katika mji

Mwandishi anaongelea kwa njia ya jumala juu ya watu wote, lakini ilikuwa ni juu ya watu wote wanaoweza kupigana.

Waliuacha mji

"Waliuacha mji ukiwa hauna ulinzi kabisa" au " baada ya kutoka, kulikuwa hakuna mtu yeyote wa kuulinda mji"

Joshua 8:18

nitaitia Ai mikononi mwako.

Kuiweka Ai katika mkono wa Israeli ina maana ya kuipa Israeli ushinid na utawala juu ya Israeli.

Joshua 8:24

baada ya Israeli walipokuwa wamemaliza kuuwaua wenyeji ... baada ya wao wote... walipokuwa wamekwisha kulala kwa ncha ya upanga

Mwandishi anatumia sentens hizi, ambazo zote zina maana moja, zikiwa na maana ya Israeli walikuwa wamelitii agizo la Mungu la kumwua kila mtu huko Ai.

walikuwa wameanguka kwa makali ya upanga

Hapa maana ya kuanguka ni kufa, na makali ya upanga yanamaanisha vita au jeshi la Israeli.

elfu kumi na mbili

"12,000"

Joshua 8:27

mahali palipoachwa ukiwa

Ni sehemu ambapo watu walioishi hapo kwanza, lakini sasa hakuna mtu aishiye hapo.

Joshua 8:29

hata leo

"leo" au "hata sasa"

Joshua 8:30

Mlima Ebali

Ni mlima ulioko huko Kanaani.

Joshua 8:34

Halikusalia hata neno moja katika yote ambayo Musa alimwagiza Yoshua ambalo halikusomwa

Maneno haya yaweza kuelezwa kwa kauli kubalifu kama "Yoshua alisoma kila neno kati ya yote ambayo Musa aliyaagiza" au "Yoshua aliisoma sheria yote ya Musa."

Israeli

Neno hili linalirejelea taifa la Israeli

Joshua 9

Joshua 9:1

Yordani

Jina la Mto Yordani

chini ya amri moja

amri hapa inamwakilisha mtu yule aliyewaamrisha. Kuwa chini yake ina maana ya kutii amri yake. "Kutii amri ya kiongozi mmoja."

Joshua 9:3

mpango wa udanganyifu

mpango wa uongo ulikusudia kuwahada Yoshua na Waisraeli.

mikavu na yenye uvundo

"kavu na iliyojaa fangasi" au iliyochina na kuharibika"

Joshua 9:6

Watu wa Israeli

inalirejelea taifa lote la Israeli

Wahivi

Hili ni jina jingine la Wagibeoni

Huenda mnaishi karibu nasi. Twawezeje kufanya agano nanyi?

Yoshua anatia mkazo kuwa watu wa Israeli lazima wafuate amri ya yahweh juu ya vitu vyote. "kama mnaishi karibu nasi, hatuwezi kufanya agano nanyi"

Joshua 9:9

Yordani

Hili ni jina la Mto Yordani

Sihoni

Hili ni jina la Mfalme wa Waamori aliyeshindwa.

Heshiboni

Hili ni jina la mji wa kifalme wa taifa la Moabu.

Ogu

Hili ni jina la mfalme wa Bashani aliyeshindwa

Ashitarothi

Hili ni jina la mji uliojulikana kwa kuabudu mungu mke aliyeitwa kwa jina hilo hilo.

Joshua 9:11

mkononi mwako

Kifungu hiki cha maneno kina maana ya "kuchukua" Neno 'mkono' linamaanisha kumiliki vitu vya Wagibeoni.

mkutane nao na muwaambia

Neno 'nao' linawarejelea watu wa Israeli.

Joshua 9:14

Yoshua akafanya amani pamoja nao na kufanya agano pamoja nao ili waishi. Viongozi wa watu nao pia wakawaapia

Sentensi hizi mbili zinaongelea juu ya jambo lile lile lililotokea. Yoshua, kiongozi wa taifa aliahidi kutowaua Wagibeoni. Viongozi wa taifa la Israeli, hivyo hivyo walifanya agano. "Yoshua na viongozi wa Israeli walifanya agano la damu na watu wa Gibeoni."

watu

Neno hili hapa linawarejelea watu wa Israeli.

Joshua 9:16

siku tatu

inarejelea namba tatu katika mpangilio

Kefira

Huu ni mmoja kati ya miji ya Wagibeoni.

Beerothi

Hili ni jina la mahali.

Kiriathi Yearimu

Hili ni jina la mahali.

Joshua 9:18

watu

Neno hili hapa linamaanisha taifa la Israeli.

Joshua 9:20

Wagibeoni wakawa wakata kuni na wachota maji

"Wagibeoni wakawa wakata kuni na wabeba maji."

Joshua 9:22

nyumba ya Mungu wangu

Maneno haya hapa yana maana ya sehemu ya Yahweh ya kukaa, yaani Hema la kukutania.

Joshua 9:24

Chochote kilicho chema na haki

Maneno 'chema' na 'haki' yanamaanisha kimsingi kitu kile kile. "chochote kilicho sawa na haki"

Joshua 9:26

aliwafanyia

neno hili linawarejelea Wagibeoni.

hadi leo

Kirai "hadi leo" kina maana ya wakati ambao mwandishi alikuwa anaishi. "hata sasa"

Joshua 10

Joshua 10:1

Ikawa

Neno hili limetumika hapa kuonesha pumziko katika mtiririko wa masimulizi ya habari. Hapa mwandishi anaongelea mtu mpaya katika habari, Adonizedeki.

Adonizedeki

Hili ni jina la kiume la mfalme muhimu

Joshua 10:3

Yarmuthi

Hili ni jina la mji

Lakishi

Hili ni jina la mji

Egloni

Hili ni jina la mji

Hohamu...Piramu...Yafia... Debiri

Haya ni majina ya wafalme

Njooni kwangu

Yerusalemu ni mji ulioinuliwa sana kuliko miji mingine ya Kanaani. "Safirini mje hapa nilipo"

Joshua 10:5

Yarmuthi

Hili ni jina la mji

Lakishi

Hili ni jina la mji

Egloni

Hili ni jina la mji

Joshua 10:6

Walisema

Kiwakilishi 'wa' kinawarejelea Wagibeoni.

Msiuondoe

Hili ni ombi la upole lililoelezwa kwa kauli hali lakini likitegemea tendo chanya.

mikono yenu

Neno 'mkono' lina maana ya nguvu za watu wa Israeli. "Tumia nguvu zako kutulinda sisi."

Joshua 10:8

Nimewatiwa wote katika mkono wako

Hapa neno "mkono" linawakilisha nguvu za watu wa Israeli na uwezo wao wa kuwashinda maadui zao.

Joshua 10:9

Yoshua aliwafikilia

Jina Yoshua, kamanda wao, limetumika hapa kuonesha Jeshi lote la Israeli.

Bethi Horoni

Hili ni jina la sehemu

Azeka...Makeda

Haya ni majina ya sehemu

Joshua 10:11

alitupa mawe makubwa kutoka mbingun

"kutupa mawe makubwa ya mvua kutoka mawinguni"

Joshua 10:12

Jua lisimame katika Gibeoni, na mwezi, usimame katika bonde la Aijalon

Yoshua anaomba kwamba Yahweh angefanya mwendelezo wa muda ukome katika siku hii.

jua...mwezi

Yoshua analiagiza jua na mwezi kana kwamba walikuwa ni watu.

Bonde la Aijaloni

Hili ni jina la mahali

Joshua 10:13

taifa

Hili linarejelea watu wa Israeli.

Je hili halikuandikwa katika Kitabu cha Yashari

Mwandishi anatumia swali hili kama usuli kuwakumbusha msomaji kwamba tukio hilo ni vizuri kumbukumbu. Katika: 'hii imeandikwa katika Kitabu cha Yashari'

Joshua 10:15

Makeda

Hili ni jina la mji

Taarifa zilimfikia Yoshua

Wajumbe walikuja na kumwambia Yoshua. "Mtu fulani alimwambia Yoshua."

Joshua 10:18

katika mkono wenu

Maneno haya "katika mkono wenu" hapa yana maana ya "utawala wako"

Joshua 10:20

Makeda

Hili ni jina la mahali

Na hakuna hata mmoja aliyethubutu kusema hata neno moja kinyume na watu wa Israeli.

Hapa "neno moja" linaongelea juu ya maadui wa Israeli. "Hakuna hata mmoja aliyethubutu kulaumu au kupinga kinyume"

Joshua 10:22

Yarmuthi...Lakishi... Eguloni

Haya ni majina ya sehemu

Joshua 10:24

Kila mtu wa Israeli

Kila askari jeshi wa Israeli

Joshua 10:26

hadi leo

mpaka mwandishi alipoandika habari hii

Joshua 10:28

Aliwateketeza wote kabisa pamoja na kila kiumbe hai kilichokuwa huko. Hakuna hata mmoja aliyesalia.

Sentensi ya pili ni fupisha sentensi na kutia mkazo kwamba Yoshua hakumwacha hai mtu au mnyama yeyote.

Joshua 10:29

Libna

Hili ni jina la mji

aliitia katika mkono wa Israeli

hapa neno 'mkono' una maana ya "kutawala" "Aliwapa Israeli utawala dhidi yao"

Joshua 10:31

Libna... Lakishi

Haya ni majina ya miji muhimu

katika mkono wa Israeli

Kauli hii ina maana ya "kuwata utawala kwa taifa la Israelil." "Bwana aliiweka Lakishi chini ya utawala wa Israeli

Joshua 10:33

Horamu

Hili ni jina la kiume la mfalme

Gezeri

HIli ni jina la mji

Joshua 10:34

Egloni

Hili ni jina mji

Waliupiga kwa upanga na waliteketeza kila mtu ndani yake

Sentensihizi zina maana moja. kwa pamoja vinaonesha utimilifu

Lakishi

Hili ni jina la mji

Joshua 10:36

Egloni

Hili ni jina la mji

aliuteka mji na kuwaua kwa upanga

upanga unawakilisha jeshi la Israeli, na kitendo cha kuwapiga na kuna maana ya kuwachinja

Waliuteka mji na kuwaua kwa upanga watu wote ndani yake pamoja na mfalme wake, kujumuisha na vijiji vyote vilivyoizunguka. Waliteketeza kabisa kila kiumbe hai ndani yake, hawakuacha hata mtu mmoja aliyesalia

Sentensi hizi mbili zinazungumzia kimsingi maana moja, na zimeunganishwa ili kutia mkazo. Kwa pamoja zinatia mkazo na kuonesha ukamilifu wa uharibifu.

Joshua 10:38

Debiri

Hili ni jina la mji

Waliwaua wote kwa upanga

Neno 'upanga' linawakilisha jeshi la Israeli na kuwaua ina maanya ya wazo la kuwaua na kuwaharibu.

Joshua 10:40

Hakuna hata mfalme moja aliyebaki hai kati ya wafalme wake wote

virai hivi viwili vina maana sawa na vinatia mkazo juu uharibifu halisi ambao watu Israeli walikuwa wameagizwa naYahweh.

Yoshua aliwaua kwa upanga

upanga unawakilisha jeshi la Israeli na kuwaua ina maanaya wazo la kuwaua na kuwaharibu.

Joshua 11

Joshua 11:1

Yabini...Yobabu

Haya ni majina ya wafalme

Ashafu...Kinerethi...Dori...Mlima Hermoni

Haya ni majina ya mahali

Hazori...Madoni...Shimuroni...Akshafu...Kinerethi...Dori ...Mlima Hermoni

Haya ni majina ya mahali

Joshua 11:4

Maelezo ya jumla

Wafalme wa Kanaani wamshambulia Yoshua na taifa la Israeli.

wanajeshi wengi sana, hesabu yao ilikuwa kama mchanga wa pwani

Maneno haya ya kutia chumvi yanatia mkazo kwamba jeshi lilikuwa kubwa lenye watu wengi sana ambalo wafalme hawa walilikusanya.

Meromu

Hili ni jina la sehemu/mahali

Joshua 11:6

ninawatia hao kwa Waisraeli wakiwa wafu

Yahweh anaiwezesha Israeli kulishinda jeshi la adui na kuwaua wanajeshi wote, na inaongelewa kana kwamba Yahweh ndiye aliyewaua wanajeshi na kisha akawatia kwa Waisraeli. "NItaiwezesha Israeli kuwaua wote katika vita."

Utaivunja vunja miguu ya farasi zao

"kuifanya farasi zao kuwa kilema kwa kuivunja miguu yao." Tendo hili ni la kukata misuli ya nyuma ya miguu ili farasi wasiweze kutembea.

Meromu

Hili ni jina la Mahali/sehemu

Joshua 11:8

Yahweh akawatia maadui katika mkono wa Israeli

Hapa neno "mkono" linawakilisha nguvu. Yahweh analiwezesha jeshi la Israeli kuwashinda maadui zao, kitendo hiki kinasemwa kana kwamba Yahweh aliwaweka jeshi la maadui katika mkono wa waisraeli.

waliwapiga kwa upanga...Waliwaua wote

Hapa neno "upanga" unawakilisha silaha zote zilizotumika kuwashambulia adui zao.

Misrefothi - Maimu

HIli ni jina la sehemu/mahali

Alivunja miguu ya farasi

Hiki ni kitendo ambacho cha kukata misuli ya nyuma ya miguu ya farasi ili farasi washindwe kukimbia.

Joshua 11:10

Alimwua mfalme wake kwa upanga

"Yoshua alimwua mfalme wa Hazori kwa upanga wake"

Hazori ulikuwa ni kichwa cha falme hizi zote

Mji wa Hazori ni mji muhimu, unatajwa kama kichwa cha falme zingine.

Waliwapiga kwa upanga kila kiumbe chenye uhai kilichokuwa huko, na alivitenga ili viteketezwe, hivyo hapakuwa na kiumbe hai kilichoachwa hai

Virai hivi viwili vina maana sawa na vinatilia mkazo kuwa maangamizi halisi.

alivitenga ili viteketezwe

Kiwakilishi 'a' kinamwakilisha Yoshua na kinajumuisha jeshi lote ambalo alikuwa akiliongoza. Walikiteketeza kabisa kila kitu kilicho hai katika mji. Vitu hivi vinasemwa kana kwamba viliwekwa wakfu ili viteketezwe.

Joshua 11:12

akawapiga wote kwa upanga

"Aliwauwa"

miji iliyojengwa juu ya vilima vya vifuasi vya udongo

"miji iliyojengwa juu vilima vidogo"

Joshua 11:14

kwa ajili yao wenyewe

Kirai hiki kinarejelea juu ya jeshi la Israeli.

Waliua kila mtu kwa upanga hadi pale walipokufa wote. Hakuna kiumbe hai kilichoachwa hai

Virai hivi viweili vina maana sawa na vinatilia mkazo juu ya uharibifu halisi

Yoshua hakuacha kufanya hata jambo moja

Kauli hii ya kukanusha inatilia mkazo kwamba Yoshua alifanya kili kitu ambacho Yahweh alimwagiza.

Joshua 11:16

Mlima Halaki...Baali Gadi

Haya ni majina ya sehemu/mahali

Joshua 11:18

Yahweh ambaye alikuwa ameifanya kuwa migumu mioyo yao

Yahweh aliwasababisha watu wa miji kuwa wakaidi, inasemwa kana kwamba Yahweh ndiye alikuwa ameifanya mioyo yao kuwa migumu.

Joshua 11:21

Anakimu

Hawa walikuwa ni wazawa wa Anaki

Debiri... Ababu

Haya ni majina ya sehemu/mahali

Joshua 11:23

Yoshua aliwapa Israeli kama urithi

Kitendo cha Yoshua kuwapa waisraeli nchi kunasemwa kana kwamba alikuwa amewapa Israeli urithi kama mali ya kudumu.

nchi ikapumzika bila vita

Watu walikuwa wahapigani vita tena, nchi inasemwa kana kwamba alikuwa ni mtu aliyepumzika kutoka katika vita. "Watu hawakupigana vita tena katika nchi" au "kulikuwa na amani katika nchi"

Joshua 12

Joshua 12:1

Basi

Neno hili limetumika hapa kuonesha pumziko katika habari kuu. Hapa mwandishi anaanza kutoa maneno ya nyuma.

hawa ni wafalme

inawarejelea orodha ya wafalme na inaendelea mpaka katika mstari wa 24

Araba... Aroeri

Haya ni majina ya mahali/sehemu

Sihoni... Heshiboni

Tafsiri maneno haya kama vile ulivyofanya katika 9:9

Joshua 12:3

Bahari ya Kinerethi

Hii ni sehemu. Tafsiri kama vile alivyofanya katika 11:1

Bethi Yeshimothi... Mlima PIsiga... Ashitarothi..Edrei..Saleka.

Haya ni majina ya sehemu/mahali

Ogu, mfalme wa Bashani

Tafsiri maneno haya kama vile ulivyofanya katika 9:9

Refaimu... Wamakathi

haya yalikuwa majina ya makundi ya watu

Joshua 12:6

Waerubeni

Hawa walikuwa wazawa wa Rubeni

Wagadi

Hawa walikuwa wazawa wa Gadi

nusu ya kabila la Manase

Wanaitwa nusu ya kabila kwasababu nusu nyingine ya kabila walipewa urithi wao katika nchi ya Kanaani.

Joshua 12:7

Baali Gadi..Mlima Halaki...Araba

Haya ni majina ya sehemu/mahali

Joshua 12:9

Enaimu...Yarmuthi...Lakishi...Eguloni..Gezeri

Haya ni majina ya miji. Tafsiri "Yarmuthi, Lakishi na Eguloni" kama ulivyofanya katika 10:3

Joshua 12:13

Debiri... Gederi...Horma..Aradi...Libna...Adulamu...Makeka

Haya ni majina ya miji

Joshua 12:17

Tapua..Heferi...Afeki...Lasharoni...Madoni...Hazori...Shimroni Meroni..Akshafu

Haya ni majina ya miji

Joshua 12:21

Taanaki...Megido...Kedeshi...Yokneamu...Dori...Goyimu......Tiriza

Haya ni majina ya miji

thelathini na moja kwa ujumla

"31 kwa ujumla"

Joshua 13

Joshua 13:2

Nchi iliyosalia ndio hii

Unaweza kuifafanua kwamba nchi ya Israeli ilikuwa bado inahitaji.

Shihori

Hili ni jina la mahali

inayofikiriwa kuwa ni mali ya Wakanaani;

Kauli hii inawezaa kuelezwa kwa muundo tendaji. "ambayo Wakanaani hufikiri kuwa ni mali yao."

Waavi

Hili ni jina la kikundi

Joshua 13:4

Meara...Afeki...Baali Gadi...Mlima Hermoni

Haya ni majina ya sehemu

Wagebali

Hili ni jina la kikundi cha watu walioishi huko Geba.

Joshua 13:6

Misrefothi Maimu

Jina la mahali

nchi ....kama urithi

Nchi ambayo Israeli wataichukua inasemwa kuwa kama ilikuwa urithi ambao wataupokea kama mali ya kudumu.

Joshua 13:8

Aroer...Medeba...Diboni

Haya ni majina ya mahali

bonde

sehemu ya mto iliyo ya chini sana kutoka usawa wa nchi katika kingo zake.

nyanda

nchi tambarare juu ya mto

Joshua 13:10

Heshiboni...Saleka... Ashitarothi...Edrei

Haya ni majina ya sehemu/mahali

Maakathi...Refaimu

Haya ni majina ya makundi ya watu

Mkoa wa Wageshuri

"nchi ambayo Wageshuri waliishi"

Musa aliwapiga

Hapa "Musa" inawakilisha jeshi la Waisraeli ambalo Musa aliliongoza. "Musa na Waisraeli waliwashambulia."

Joshua 13:13

Wageshuri au Wamakathi

Haya ni majina ya makundi ya watu

Wageshuri na Wamakathi wanaishi miongoni mwa Waisraeli

"Geshuri" na "Makathi" ni majina ya waanzilishi au mababu wa Wageshuri na Wamaakathi au ni majina ya miji walioishi. "Watu wale waliishi kati ya Waisraeli.

hadi leo

hii inarejelea kipindi ambacho mwandishi alikuwa akiandika.

Joshua 13:14

halikupewa urithi na Musa

Nchi ambayo Musa aliyapa makabila ya Israeli inasemwa kana kwamba ulikuwa ni urithi ambao watu waliupokea kama mali ya kudumu.

Urithi wao ni sadaka za Yahweh

Mwandishi anaongelea juu ya heshima kubwa ambayo Walawi walikuwa nayo ya kumtumikia Yahweh kama makuhani na ya kwamba sadaka zingekuwa urithi wao.

sadaka za Yahweh

"sadaka ambazo watu walizileta kwa Yahweh"

zilitolewa kwa moto

kauli hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "ambazo makuhani walizichoma kwa moto"

Joshua 13:15

Aroeri...Medeba

Haya ni majina ya sehemu/mahali

bonde... nyanda

Tafsiri manen haya kama ulivyofanya katika 13:8

Joshua 13:17

Heshiboni...Diboni...Bamothi...Baali... Bethi Baalimeoni...Yahazi....Kedemothi....Mefathi... Kiriathaimu.......Sibuma...Zerethishahari.

Haya ni majina ya sehemu/mahali

Joshua 13:20

Bethi Peori...Pisiga..Bethi Yeshimothi...Heshiboni

Haya ni majina ya sehemu/mahali

Sihoni...Evi...Rekemu...Zuri...Huri...Reba

Haya ni majina ya watu

pamoja na viongozi wa Midiani

"kama ambavyo alikuwa amewashinda viongozi wa Midiani"

Joshua 13:22

huu ni mpaka wao

Mto Yordani ulikuwa mpaka upande wa magharibi wa nchi ambayo kabila la Reubeni waliipokea.

Huu ulikuwa urithi wa kabila la Rubeni

Nchi ambayo Musa aliwagawia kabila la Rubeni inazungumziwa kana kwamba ilikuwa ni urithi ambao kabila la Rubeni walipokea kama mali ya kudumu.

uliotolewa kwa kila ukoo,

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji: "ambao Musa aliwapa kila ukoo."

Joshua 13:24

Yazeri...Aroeri...Heshiboni...Ramathi Mizipe...Betonimu...Mahanaimu...Debiri

Haya ni majina ya mahali

Joshua 13:27

Bethi Haramu...Bethi Nimra....Zafoni....Heshiboni

Haya ni majina ya mahali/sehemu

Huu ni urithi wa kabila la Gadi

Nchi ambayo Musa aliwagawia kabila la Gadi inazungumziwa kana kwamba ilikuwa ni urithi ambao kabila la Gadi walipokea kama mali ya kudumu.

Joshua 13:29

Musa aliwapa urithi nusu ya kabila la Manase

Nchi ambayo Musa aliwapa nusu ya kabila la Manase inazungumziwa kana kwamba ulikuwa ni urithi ambao aliwapa kama mali ya kudumu.

nusu ya kabila la Manase

Ni nusu tu ya kabila ilipokea nchi hii kwasababu nusu nyingine ilipokea nchi katika upande mwingine wa mto Yordani.

Uligawiwa

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Musa aliugawa"

Mahanaimu...Yairi...Ashitarothi...Edrei.

haya ni majina ya mahali/sehemu

Makiri

Hili ni jina la mwanaume.

hii iligawanywa

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Musa alizigawa hii miji"

Joshua 13:32

Huu ni urithi ambao Musa aliowagawia

Nchi ambayo Musa aliyagawia makabila ya Israeli upande wa mashariki wa mto Yordani unazungumziwa kana kwamba ilikuwa ni urithi ambao Musaaliwapakama urithi.

Yahweh, Mungu wa israeli, ni urithi wao

Mwandishi anazungumzia juu ya heshima kubwa ambayo Walawi walikuwa nayo kwa kumtumikia Yahweh kama makuhani kana kwamba Yahweh kilikuwa ni kitu fulani ambacho watarithi.

Joshua 14

Joshua 14:1

Maeneo haya ya nchi ambayo watu wa Israeli waliyapokea kama urithi wao

Nchi ambayo waisraeli waliipata inazungumzwa kana kwamba ilikuwa ni urithi ambao waliupata kama mali ya kudumu.

Urith huu uligawanywa kwao na Eliazeri kuhani, na Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa makabila ya mababu wa familia zao kati ya watu wa Israeli

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "ambao Eliazeri kuhani , mwana wa Yoshua mwana wa Nuni na viongozi wa makabila ya familia za mababu zao katika Israeli waliwapa."

Viongozi wa makabila

Hawa walikuwa viongozi wa kila kabila

Joshua 14:2

Urithi wao ulichaguliwa kwa kupiga kura

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. Eliazeri, Yoshua na viongozi wa makabila walipiga kura kuamua urithi wao."

kwa mkono wa Musa

Hapa neno "mkono" unamwakilisha Musa mwenyewe na ina maana ya Yahweh alimtumia Musas kama wakala ili kutoa agizo hili.

Musa alikuwa amewapa urithi makabila mawili na nusu ng'ambo ya Yordani, lakini Walawi hawakupewa urithi wowote

Makabila mawili na Nusu yalipewa urithi ng'ambo ya Yordani, lakini kwa Walawi hawakupewa urithi wowote. Nchi ambayo Musa aliyapa makabila inasemwa kana kwamba ni urithi ambao walipokea kama miliki yao ya kudumu.

Na hakuna sehemu yoyote ya urithi waliyopewa Walawi katika nchi

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Na Musa hakuwapa sehemu yoyote ya urithi kwa Walawi katika nchi."

sehemu ya nchi

Kipande cha ardhi

lakini walipewa miji ya kuishi ndani yake

Kitenzi huenda kimetolewa kwa maelezo yaliyotangullia."lakini aliwapa miji fulani ili kuishi ndani yake."

maeneo ya malisho

haya ni mashamba ya nyasi kwa ajili kulishia mifugo.

riziki zao

hivi ni vitu walivyohitaji ili waweze kuhudumia familia zao.

Joshua 14:6

Yefune

Hili ni jina la mwanaume

Mkenizi

Hili ni jina la kikundi cha watu

Nilimletea taarifa tena kama nilivyotakiwa kufanya katika moyo wangu.

Hapa neno "moyo" linawakilisha mawazo. Hii ni nahau inayorejelea taarifa iliyotolewa kwa uadilifu.

Joshua 14:8

waliifanya mioyo ya watu iyeyuke kwa woga

Kitendo cha kuwafanya watu waogope kinaongelewa kama ilikuwa ni kuyeyusha mioyo ya watu.

Lakini mimi nilimfuata Yahweh kabisa

Kuwa mwaminifu kwa Yahweh kunaongelewa kama kumfuata Yahweh. "Nilibaki mwaminifu kwa Yahweh"

nchi ambayo miguu yako imetembea juu yake itakuwa urithi wako na kwa watoto wako milele

Nchi ambayo Kalebu na watoto wake wangepewa inaongelewa kana kwamba ni urithi ambao wangeupokea kama miliki ya kudumu.

nchi ambayo miguu yako imetembea juu yake

hapa maneno "miguu yako" inamwakilisha Kalebu.

Joshua 14:10

Tazama

"Sikiliza" Neno hili linaongeza mkazo kwa kile kilichosemwa baadaye.

wakati huo Waisraeli walikuwa wakitembea jangwani

"Wakati watu wa israeli walisafiri huko jangwani"

Nguvu zangu za sasa ni sawa na nguvu zangu za kipindi kile

"Bado nina nguvu sasa kama nilivyokuwa hapo mwanzo."

kwa kwenda na kwa kuja.

Hii ni nahau inayorejelea shughuli za kila siku. "Kwa ajili ya mambo ninayoyafanya kila siku."

Joshua 14:12

nchi ya milima

Maana zinazokubalika a) vilima vingi vikubwa au milima midogo au b)mlima mmoja.

Anakimu

Hili ni jina la kikundi cha watu

Joshua 14:13

alimpa Hebroni kama urithi wake

Hebroni inaongelewa kana kwamba ulikuwa ni urithi ambao Kalebu aliupokea kama mali ya kudumu.

hata leo

hii inarejelea kipindi ambacho mwandishi wa kitabu hiki

alimfuata kabisa Yahweh,

Kuwa mwaminifu kwa Yahweh kunatajwa kana kwamba kumfuata Yahweh kweli kweli. "Alibaki akiwa mwaminifu kwa Yahweh"

Kiriathi Arba

Hili ni jina la mahali/sehemu

Kisha nchi ikawa na raha bila vita.

Watu walikuwa hawapigani vita tena. Hali hii inaangaliwa kama nchi kupumzika kama vile mtu anavyopumzika kutoka katika vita.

Joshua 15

Joshua 15:1

Sini

Hili ni jina la sehemu ya jangwa

ghuba

sehemu ndogo ya ziwa ambayo imeingia katika sehemu ya nchi kavu

ulianzia mwisho wa Bahari ya Chumvi, kutoka ghuba iliyokabili upande wa kusini

"kutoka katika ghuba iliyokabili upande wa kusini sehemu ya mwisho ya Bahari ya Chumvi" Virai hivi viwili vya maneno vinarejelea sehemu moja. Kirai cha pili kinafafanua sehemu unapoanzia mpaka wa kusini.

iliyokabili upande wa kusini

"ambayo imegeukia kuelekea kusini"

Joshua 15:3

Mpaka wao

"Mpaka wa nchi iliyo mali ya kabila la Yuda"

Akirabimu...sini....Hebroni... Addari...Karka...Azimoni

Haya ni majina ya sehemu/mahali

kijito cha Misri

huu ni mto mdogo wa maji katika ukingo wa upande wa kusini magharibi mwa nchi, karibu na Misri.

Joshua 15:5

katika mdomo wa Yordani

Sehemu ambayo mto humwaga maji yake baharini inazungumzwa kana kwamba ulikuwa ni mdomo wa mto.

mpaka...ulianzia

"mpaka...ulikuwa"

Bethi Hogla...Bethi Araba

haya ni majina ya sehemu/mahali

JIwe la Bohani

Hili lilikuwa ni jiwe kubwa lililowekwa na mtu fulani kama alama ya mpaka na liliitwa kwa jina la mtu aliyeitwa Hohani.

Joshua 15:7

Debiri...bonde la Akori...mlima wa Adumimu..En shemeshi... En Rogeli...bonde la Ben Hinnomu..Bonde la Refaimu

Haya ni majina ya sehemu/mahali

Joshua 15:9

Nefutoa..Mlima Efroni...Baala..Kiriathi Yearimu..Mlima Seiri..Mlima Yearimu.... Kesaloni...Bethi Shemeshi...Timna.

Haya ni majina ya sehemu/mahali

Joshua 15:11

Shikeroni...Mlima baala...Yabuneeli

Haya ni majina ya sehemu/mahali

Joshua 15:13

Kiriathi Arba...Debiri...Kiriathi Seferi

Haya ni majina ya sehemu/mahali

Arba...Anaki...Sheshai...Ahimani...Talmai

Haya ni majina ya watu

wana watatu wa Anaki: Sheshai, Ahimani na Talmai, wazawa wa Anaki

Majina haya yanawakilisha koo za watu ambao walikuwa ni uzao wa Sheshai, Ahimani, na Talmai. Maneno "wana' na "wazawa" katika muktadha huu yanamaanisha kitu hicho hicho kimoja. "Koo tatu , Sheshai, Ahimani na Talmai, waliokuwa wazawa wa Anaki."

Alipanda kutoka pale kinyume

"Alienda kutoka hapo ili kupigana dhidi"

Joshua 15:16

Kiriathi Seferi

Hili ni jina la sehemu/mahali

Akisa

Hili ni jina la mwanamke

othinieli ...Kenazi

Haya ni majina ya wanaume.

Joshua 15:18

Akisa alienda kwa Othinieli

Hii ni nahau ambayo inamrejelea Akisa kuwa mke wa othinieli. "Wakati Akisa alipokuwa mke wa Othinieli."

alimsihi amwombe baba yake shamba

Hii inaweza kutafsiriwa kama kauli ya moja kwa moja. 'alimsihi, 'mwombe baba yangu anipe shamba"

Joshua 15:19

chemichemi ya juu na chemichemi ya chini

Maneno "juu" na "chini" yanaongelea masuala ya mwinuko wa kijiografia katika sehemu za vijito vya maji.

Joshua 15:20

Huu ulikuwa ndio urithi wa kabila la Yuda,

Nchi ambayo kabila la Yuda lilipokea inaongelewa kana kwamba ulikuwa ni urithi ambao waliupata kama mali ya kudumu.

waliopewa kufuatana na koo zao

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "ambayo Yoshua aliwapa kwa koo zao"

Joshua 15:21

Sentensi kiunganishi

mwandishi anaorodhesha miji ya kusini ambayo Yuda waliimiliki. Orodha inaendelea mpaka 15:29

Joshua 15:25

Maelezo unganishi

Orodha ya miji inaendelea

Joshua 15:29

maelezo unganishi

Orodha ya miji inaendelea

Joshua 15:33

Maelezo ya jumla

Mwandishi anaorodhesha miji ya upande wa Kaskazini ambayo Yuda iliimiliki.

Joshua 15:37

sentensi kiunganishi

Mwandishi anaorodhesha miji ambayo Yuda ilipewa kuimiliki

Joshua 15:40

Sentensi kiunganishi

Mwandishi anaorodhesha miji ambayo Yuda ilipewa kuimiliki

Joshua 15:42

Sentensi kiunganishi

Mwandishi anaorodhesha miji ambayo Yuda ilipewa kuimiliki

Joshua 15:45

Sentensi kiunganishi

Mwandishi anaorodhesha miji ambayo Yuda ilipewa kuimiliki

makazi

"vijiji"

Kijito cha Misri

Mto mdogo wa maji katika ukingo wa upande wa kusini wa nchi karibu na Misri.

Joshua 15:48

Sentensi unganishi

Mwandishi anaorodhesha miji ambayo Yuda ilipewa kuimiliki

Joshua 15:52

Sentensi unganishi

Mwandishi anaorodhesha miji ambayo Yuda ilipewa kuimiliki

Joshua 15:55

Sentensi unganishi

Mwandishi anaorodhesha miji ambayo Yuda ilipewa kuimiliki

Joshua 15:58

Sentensi unganishi

Mwandishi anaorodhesha miji ambayo Yuda ilipewa kuimiliki

Joshua 15:60

Sentensi unganishi

Mwandishi anaorodhesha miji ambayo Yuda ilipewa kuimiliki

Joshua 15:63

hadi leo hii

kipindi kinachorejelewa hapa ni kipindi ambacho mwandishi aliandika kitabu hiki.

Joshua 16

Joshua 16:1

Kabila la Yusufu

Kabila la Yusufu liliunganisha makabila ya wana wake wawili, Manase na Efraimu. Kwakuwa nusu ya kabila la Manase lilikuwa limeweka makazi mashariki mwa Yordani, sehemu hii inarejelea kabila la Efraimu na nusu nyingine ya kabila la Manase.

Luzi ...Atarothi

Haya ni majina ya mahali

Waarkiti

hili ni jina la kikundi cha watu

Joshua 16:3

Wayafuleti

Hili ni jina la kikundi cha watu

Loweri Bethi Horoni ... Gezeri

haya ni majina ya sehemu

makabila ya Yusufu, Manase na Efraimu

"makabila ya Manase na Efraimu, wana wa Yusufu"

waliupokea uirithi wao

Nchi ambayo makabila ya Manase na Efraimu waliimiliki inasemwa kana kwamba ulikuwa ni urithi ambao waliupokea kama mali ya kudumu.

Joshua 16:5

Eneo la kabila la Efraimu ambalo lilikuwa limegawanya kwa koo zao

Sentensi hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Eneo ...ambalo Yoshua aliwagawia kwa kufuata koo zao."

Atarothi Addari...Bethi Horoni ya juu...Mikimethathi...Taanathi Shilo...Yanoa...Naara

Haya ni majina ya sehemu/mahali

Joshua 16:8

Tapua...Kana

Haya ni majina ya sehemu

Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Efraimu

Nchi ambayo kabila la Efraimu waliimiliki inasemwa kana kwamba ulikuwa ni urithi ambao waliupokea kama mali ya kudumu

Walipewa kwa koo zao

Maelezo haya yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "ambayo Yoshua aliwagawia kwa koo zao"

miji yao iliyochaguliwa

Maelezo haya yaweza kuelezwa kwa kauli tendaji. Miji ambayo Yoshua alikuwa ameichagua."

iyokuwa ndani ya urithi wa kabila la Manase

Nchi ambayo kabila la Manase waliimiliki inasemwa kana kwamba ulikuwa ni urithi ambao waliupokea kama mali ya kudumu

Joshua 16:10

hadi leo

kipindi hiki kinachorejelewa hapa ni kipindi ambbacho mwandishi aliandika kitabu hiki.

Joshua 17

Joshua 17:1

mzaliwa wa kwanza wa Manase, ambaye alikuwa

"alikuwa ni mzaliwa wa kwanza"

Makiri...Abi Ezeri, Heleki, Asrieli, Shekemu, Heferi, na Shemida

Haya yalikuwa ni majina ya wanaume

Watoto wa Makiri walipewa nchi ya Gileadi na Bashani

Maneno haya yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Yoshua aliwapa nchi ya Gileadi na Bashani wazawa wa Makiri.

Nchi iliyobaki iligawiwa .... walipewa kwa koo zao

Maelezo haya yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Yoshua aliwapa nchi.... na aliwapa kwa kufuata koo zao."

Joshua 17:3

Zelofehadi...Heferi...Eliazari

Haya ni majina ya wanaume

Mahila, Noa, Hogila, Milka, na Tirsa

Haya ni majina ya wanawake.

atupatie urithi wetu

Nchi inaongelewa hapa kana kwamba ulikuwa ni urithi ambao watu walilpewa kama mali ya kudumu. "kutupa sisi sehemu ya nchi kama urithi"

aliwapa wanawake hao urithi

Maana zinazokubalika a)"Yoshua aliwapa wale wanawake urithi" b) Eliazeri aliwapa wanawake urithi.

Joshua 17:5

alipewa sehemu kumi za nchi

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Yoshua aliwapa sehemu kumi za nchi."

"sehemu kumi"

"vipande kumi"

aliupokea urithi

Nchi inaongelewa hapa kana kwamba ulikuwa ni urithi ambao watu walilpewa kama mali ya kudumu. "kutupa sisi sehemu ya nchi kama urithi"

Nchi ya Gileadi iligawanywa

Hii inaweza kuelezwa kwa kutumia muundo tendaji. "Yoshua aliwapa nchi ya Gileadi"

Joshua 17:7

Upande wa Kusini

"kuelekea kusini"

Mikimethathi ...Tapua

Haya ni majina ya mahali/sehemu

Joshua 17:9

Mpaka

"Mpaka wa nchi ya Manase"

kijito

sehemu ndogo ya mto

Kana

Jina la kijito

Kwa upande wa kaskazini ulifika hata Asheri

Maana zinakubalika ni a) mpaka wa nchi ya Manase ulifika na kugusua nchi ya kabila la Asheri b)ambayo waweza kusafiri kutoka Kaskazini na kufika Asheri.

upande wa mashariki, Isakari

Kitenzi huenda ni kile kile ambacho kimetolewa virai vilivyotangulia.

Joshua 17:11

Bethi Shani...Ibleamu...Dori...Endori...Taanaki...Megido....Nafethi.

Haya ni majina ya sehemu/mahali

Joshua 17:14

wazawa wa Yusufu

Inarejelea makabila ya Efraimu na Manase

Kwanini umetupa mgao mmoja wa nchi na sehemu moja kwa ajili ya urithi, kwa kuwa tuko wengi , na kwa muda wote Yahweh umetubaliriki?

Watu wa makabila ya Efraimu na Manase waliuliza swali hili ili kutia mkazo kwamba Yoshua alitakiwa kuwapa sehemu kubwa ya nchi. "Ulitakiwa ungekuwa umetupa sisi sehemu zaidi ya kila mtu...Yahweh ametubariki."

mgao mmoja wa nchi na sehemu moja kwa ajili ya urithi

Virai hivi viwili kwa msingi vina maana moja. Katika kirai cha pili kinahusu juu nchi inayozungumziwa kama urithi ambao watu waliupokea kama mali kudumu.

sehemu

Kipande

watu wengi

Watu wengi kwa namba

"Kama ninyi ni watu wengi katika hesabu

Kwa kuwa ninyi ni watu wengi sana katika hesabu yao.

Refaimu

Hili ni jina kikundi cha watu

Joshua 17:16

Bethi Shani....Yezreeli

Haya ni majina ya mahali/sehemu

Nyumba ya Yusufu

Hapa neno "nyumba" inarejelea wazawa

Mtaufyeka

"Mtausafisha msitu wa miti" au " mtaikata miti yake"

Joshua 18

Joshua 18:1

na waliishinda nchi

Walikuwa wamewashinda watu walioishi katika nchi kabla hawajaweka hema la kukutania.

yalikuwa bado hayajapewa urithi wao

Nchi ambayo watu watairithi inaongelewa kana kwamba ulikuwa ni urithi ambao wangeupokea kama mali yao ya kudumu.

Joshua 18:3

Je mtaacha mpaka lini katika kuingia nchi ambayo Yahweh, Mungu wa baba zenu, amewapeni ninyi?

Yoshua aliuliza swali hili ili kuwatia moyo Waisraeli kuchukua umiliki wa nchi.

nchi juu na chini

maneno "juu na chini" yana maana ya kila mwelekeo/sehemu

Wataandika maelezo pamoja na maelekezo kuhusu urithi

Hii ina maana kwamba wataeleza sehemu za nchi ambazo kila kabila lingepokea kwa ajili ya urithi.

urithi wao

Nchi ambayo watu watairithi inaongelewa kana kwamba ulikuwa ni urithi ambao wangeupokea kama mali yao ya kudumu

Joshua 18:5

Maelezo ya jumla

Yoshua anaendeleza hotuba yake kwa watoto wa israeli

Wataigawanya nchi

Wataigawa nchi

Yuda itasalia

"Kabila la Yuda litabaki"

nyumba ya Yusufu

Hapa neno "nyumba" inawakilisha wazawa wa Yusufu. Kirai kinayarejelea makabila ya Efraimu na Manase.

Joshua 18:7

Maelezo ya jumla

Yoshua anaendeleza hutoba yake kwa watoto wa Israeli.

hana sehemu

Hakuna sehemu ya nchi

kwa kuwa ukuhani wa Yahweh ni urithi wao

Yoshua anazungumzia juu ya heshima kubwa ambayo Walawi walikuwa nayo kwa kumtumikia Yahweh, ilikuwa kana kwamba ulikuwa ni urithi.

nusu ya kabila la Manase

"nusu ya kabila la Manase"

wameshapokea urithi wao

Nchi ambayo watu watairithi inaongelewa kana kwamba ulikuwa ni urithi ambao wangeupokea kama mali yao ya kudumu

Joshua 18:8

Maelezo ya jumla

Yoshua anaongea na watu Ishirini na moja ambao walitakiwa kwenda kuiangalia nchi.

Juu na chini katika nchi

Maneno "juu na chini" yana maana ya sehemu zote."Pande zote za nchi" au "katika nchi yote"

Joshua 18:10

kila kabila lilipewa sehemu ya nchi.

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "kwa kila kabila Yoshua aliwapa sehemu ya nchi"

Joshua 18:11

Katika kabila la Benyamini, ugawanaji wa nchi ulifanyika kwa kupewa kwa koo zao

Hii inaweza kuelezwa muundo tendaji. "Kila kabila la Benyamini lilipewa kwa kufuata koo zao."

ati ya wazawa wa Yuda na wazawa wa Yusufu

"kati ya nchi ambayo ni mali ya wazawa wa Yuda na nchi iliyo mali ya wana wa Yusufu."

Wazawa wa Yusufu

hii inawarejelea kabila la Efraimu na Manase.

Bethi Aveni

Hili ni jina la mahali/sehemu

Joshua 18:13

Luzi...Atarothi Addari...Bethi Horoni...Kiriathi Baali...Kiriath Yearimu.

Haya ni majina ya sehemu/mahali

Joshua 18:15

Kiriathi Yearimu...Efroni...Neftoa...Beni Hinomu...Refaimu...Hinnomu...En Rogeli

Haya ni majina ya sehemu/mahali

Joshua 18:17

Eni Shemeshi...Gelilothi...Adumimu...Bethi Araba

Haya ni majina ya sehemu/mahali

Jiwe la Bohani

Hili lilikuwa ni jiwe kubwa ambalo mtu fulani aliliweka kama alama na liliitwa kwa jina la mtu aliyeitwa Bohani.

bega la Bethi Araba

Nchi ambayo ina mteremko au mgongo ulioinama inasemwa kana kwamba ni bega. "Mteremko wa Bethi Araba"

Joshua 18:19

Bega la kaskazini la Bethi Hogla

Nchi ambayo ina muundo wa mteremko inazungumzwa kana kwamba ni bega.

Bethi Hogla

Hili ni jina la sehemu/mahali

huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Benyamini

Nchi ambayo kabila la Benyamini iliipokea inazungumzwa kana kwamba ilikuwa ni urithi wa ambao waliupokea kama mali ya kudumu.

walipewa kwa kila ukoo wao

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji: "Yoshua aliwapa nchi kwa kila koo"

Joshua 18:21

Maelezo ya jumla

Mwandishi anaorodhosha miji ambayo ilikuwa katika nchi na ambazo kabila la Benyamini walipewa kuimiliki kama urithi wao.

vijiji vyake

"Vijiji vilivyoizunguka"

Joshua 18:25

Maelezo ya jumla

Mwandishi anaendelea kuorodhoshe miji ambayo ilikuwa katika nchi na ambazo kabila ala Benyamini.

Huu ulikuwa ni urithi wa Benyamini

Nchi na miji ambayo kabila l Benyamini walipewa inaongelewa kana kwamba ilikuwa ni urithi kama mali ya kudumu.

Joshua 19

Joshua 19:1

Upigaji wa pili wa kura uliangukia kwa Simoni

"Mara ya pili Yoshua alipopiga kura, kura ilionesha kabila la Simoni"

wa pili

Namba ya pili katika orodha

waligawiwa kwa kila ukoo wao

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji: " Yoshua aligawa nchi kwa kila kabila lao"

Urithi wao ulikuwa katikati ya urithi ulikuwa ni mali ya kabila la Yuda.

Nchi waliyopewa makabila haya inazungumzwa kana kwamba ulikuwa ni urithi ambao waliupokea kama mali ya kudumu. "Nchi waliyopokea kama urithi ilikuwa katikati ya nchi ambayo kabila la Yuda walipewa kama urithi"

Joshua 19:2

Maelezo ya jumla

Mwandishi anaorodhesha miji ambayo ilikuwa katika nchi ambayo kabila la Simoni waliipokea kama urithi wao.

Urithi waliokuwa nao

Nchi na miji ambayo kabila la Simoni liliipokea inasemwa kana kwamba ulikuwa ni urithi ambao waliupokea kama mali ya kudumu.

Joshua 19:5

Maelezo ya jumla

Mwandishi anaorodhesha miji ambayo ilikuwa katika nchi ambayo kabila la Simoni waliipokea kama urithi wao.

Ziklagi

Tafasiri kama ulivyofanya katika 15;19

Joshua 19:8

Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Simon

Nchi na miji ambayo kabila la Simoni liliipokea inasemwa kana kwamba ulikuwa ni urithi ambao waliupokea kama mali ya kudumu

waliopewa kwa koo zao

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "ambayo Yoshua aliwapa kwa koo zao"

Hii ni kwasababu nchi waliyopewa kabila la Yuda

Sentensi hii inaweza kuelezwa wa muundo tendaji: "Sehemu ya nchi ambayo Yoshua aliigawa kwa kabila la Yuda"

sehemu yao ya katikati

"Katikati ya sehemu ya nchi ya Yuda"

Joshua 19:10

Upigaji wa kura ya tatu

Tafasiri kirai hiki kama vile ulivyofanya katika 19:1

ya tatu

namba ya tatu katika orodha

Saridi...Marala..Dabeshethi...Yokineamu

Haya ni majina ya sehemu/mahali

mkabala na Yokineamu

"ng'ambo ya pili kutoka Yokineamu"

Joshua 19:12

Saridi....Kisilothi Tabori....Daberathi...Yafia...Gathi Hefa...Ethikazini...Rimoni...Nea

Haya ni majina ya sehemu/mahali.

Joshua 19:14

Hannathoni...Efta Eli Katathi...Nahalali...Shimroni...Idala...Bethlehemu

Haya ni majina ya sehemu/mahali

Bethlehemu

Hii siyo ile "Bethlehemu" ambayo iko kusini mwa Yerusalemu katika Yuda.

Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Zabuloni,

Nchi na miji ambayo kabila la Zabuloni liliipokea inasemwa kana kwamba ulikuwa ni urithi ambao waliupokea kama mali ya kudumu

waliopewa kwa kufuatana na koo za

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "ambayo Yoshua aliwapa kwa koo zao"

Joshua 19:17

Upigaji kura wa nne

Tafasiri kirai hiki kama vile ulivyofanya katika 19:1

wa nne

namba ya nne katika orodha

Kesulothi...Shunemu...Hafaraimu...Shioni...Anaharathi

Haya ni majina ya mahali/sehemu

Joshua 19:20

Rabithi...Kishioni...Ebezi...Remethi...Enganimu...Enihada...Bethipazezi..Shahazuma

Haya ni majina ya mahali/sehemu

Tabori

Hili ni jina la mlima

Joshua 19:23

Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Isakari

Nchi na miji ambayo kabila la Zabuloni liliipokea inasemwa kana kwamba ulikuwa ni urithi ambao waliupokea kama mali ya kudumu

waliopewa kwa kufuatana na koo za

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Yoshua aliwapa kwa koo zao."

Joshua 19:24

Upigaji wa kura ya tano

Tafasiri kirai hiki kama ulivyofanya katika 19:1

wa tano

namba ya tano katika orodha

walipewa kwa koo zao

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "ambayo Yoshua aliwapa kwa koo zao"

Helkathi, hali, Beteni, Akshafu, Allameleki, Amadi, na Mishali..Shihori Libnathhi

Haya ni majina ya sehemu/mahali

Joshua 19:27

Bethi Dagoni...Bonde la Iftaheli...Bethimeki..Neieli..Kabuli...Ebroni...Rehobu...Hammoni ...Kana.

Haya ni majina ya sehemu/mahali

Joshua 19:29

Hosa...Akizibu...Umma... Afeki...Rehobu

Haya ni majina ya sehemu/mahali

Joshua 19:31

Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Asheri

Nchi na miji ambayo kabila la Asheri liliipokea inasemwa kana kwamba ulikuwa ni urithi ambao waliupokea kama mali ya kudumu waliopewa kwa kufuatana na koo zao

waliopewa kwa koo zao

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "ambayo Yoshua aliwapa kwa koo zao"

Joshua 19:32

Upigaji wa kura wa mara ya sita

Tafasiri kirai hiki kama ulivyofanya katika 19:1

ya sita

namba ya sita katika orodha

walipewa kufuatana na koo zao

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "ambayo Yoshua aliwapa kwa koo zao

Helefu...Zaananimu...Adaminekebu...Yabuneeli...Lakumu...Zazinothi Tabori Hukkoki

Haya ni majina ya miji

Joshua 19:35

Ziddimu...Zeri...Hamathi..Rakathi...Kinerethi...Adama...Raa..Hazori...Edrei...Eni Hazori

Haya ni majina ya miji

Hamathi

Hii si lile eneo la "Hamathi" bali ni eneo la upande wa magharibi mwa Bahari ya Galilaya.

Joshua 19:38

Yironi...Migdaleli..Horemu...Bethi Anathi

Haya ni majina ya miji

Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Nafutali

Nchi na miji ambayo kabila la Nafutali liliipokea inasemwa kana kwamba ulikuwa ni urithi ambao waliupokea kama mali ya kudumu,

walipewa miji pamoja na vijiji vyake kufuatana na koo zao

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "ambayo Yoshua aliwapa kwa koo zao

Joshua 19:40

Upigaji wa kura ya saba

Tafasiri kirai hiki kama ulivyofanya katika 19:1

ya saba

namba ya saba katika orodha

Eneo lao la urithi

Nchi na miji ambayo kabila la Dani liliipokea inasemwa kana kwamba ulikuwa ni urithi ambao waliupokea kama mali ya kudumu,

Zora, Eshitaoli, Iri Shemeshi, 42Shaalabini, Aijaloni, na Ithila

Haya ni majina ya mahali/sehemu

Joshua 19:43

Eloni, Timna, Ekroni, 44Eliteke, Gibethoni, Baalathi, 45Yehudi, Bene - Beraki, Gathi Rimoni, Me -Yarkoni, na Rakoni

Haya ni majina ya miji

sambamba na eneo la karibu na Yopa

"mkabala na Yopa" au "pembeni ya Yopa"

Joshua 19:47

Leshemu

Hili ni jina la mji

Huu ulikuwa urithi wa kabila la Dani,

Nchi na miji ambayo kabila la Dani liliipokea inasemwa kana kwamba ulikuwa ni urithi ambao waliupokea kama mali ya kudumu,

waliopewa kufuatana na koo zao

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "ambayo Yoshua aliwapa kwa koo zao

Joshua 19:49

walimpa urithi Yoshua mwana wa Nuni kutoka miongoni mwao

Mji ambao Yoshua alipokea unasemwa kana kwamba ulikuwa ni urithi ambao waliupokea kama mali ya kudumu

Timnathi Sera

Hili ni jina la mji

Joshua 19:51

Na huu ndio urith...waligawa

Nchi na miji ambayo makabila mbalimbali yaliipokea inasemwa kama ulikuwa ni urithi ambao waliupokea kama mali ya kudumu.

Joshua 20

Joshua 20:1

kwa mkono wa Musa

Hapa neno "mkono" linarejelea maandiko ambayo Musa aliyaandika. "kupitia mambo ambayo Musa aliyaandika"

akiua mtu bila kukusudia

Hii hutokea pale ambapo mtu humwua mtu mwingine bila kunuia kufanya hivyo.

kulipiza kisasi kwa damu ya mtu aliyeuliwa kulipiza kisasi kwa damu ya mtu aliyeuliwa

Hapa kumwaga damu ya mtu kuna maana ya kifo. Muundo tendaji unaweza kutumika."kulipiza kisasi cha kifo cha mtu"

Joshua 20:4

Atakimbilia

Hapa kiwakilishi 'a' kinamrejelea mtu yule aliyeua bila kukusudia.

na ataeleza kesi yake kwa wazee wa mji ule

"kuwashawishi wazee wa mji ule ya kwamba aliua mtu bila kukusudia.

Kisha watamwingiza

Kiwakilishi 'wa' kinawarejelea wazee na kiwakilishi "m' kinamrejelea mtu aliyeua bila kukusudia.

kuishi miongoni mwao

Hii inarejelea mji wote kwa ujumla, na si kwa wazee tu.

Joshua 20:5

kulipiza kisasi kwa damu ya mtu yule ambaye aliuliwa

Sentensi hii yaweza kutumia muundo tendaji. "kulipiza kifo cha mtu"

kumtoa

Neno hili lina maana ya kumweka mtu chini ya mtu mwingine mwenye mamlaka.

amesimama mbele ya kusanyiko

Hiki ni kirai kinachoeleza juu ya kutafuta haki kutoka katika mahakamaya kusanyiko la wananchi wenzake.

Joshua 20:7

Maelezo ya jumla

Kuna majina mengi sana katika sehemu hii

Yordani

Hili ni jina la Mto Yordani

Joshua 20:9

Mtu huyu hatakufa kwa mkono wa mtu yule

Hapa neno "mkono" lina maana kwamba mtu huyu atakuwa mhanga au mtendwa wa moja kwa moja wa mtu aliyemwua mkimbizi

kulipiza kisasi cha damu iliyomwagw

Hii inaweza kuelezwa kwa kutumia muundo tendaji. "kulipiza kifo cha mtu"

Joshua 21

Joshua 21:1

Eliazari...Nuni

Haya ni majina ya watu

Waliwaambia

"Walawi wakawaambia"

Yahweh aliwaagizeni ninyi kwa mkono wa Musa

Kirai "kwa mkono wa" kina maana kwamba Yahweh alimtumia Musa kama chombo ili kuleta agizo lake.

Joshua 21:3

miji ifuatayo

Hii inarejelea miji ambayo itaorodheshwa kwenye mstari unaofuata.

Joshua 21:4

Upigaji wa kura

Hii ni njia ya kuchagua ambayo ilikuwa ya kubahatisha yaani bila mpango maalumu ili kuondoa utashi wa viongozi, mara kwa mara ilifanywa kwa wazo kuwa Mungu ataamua matokeo.

Wakohathi

Makuhani hwa katika kundi hili walikuwa ni wazao wa Mwana wa Lawi aliyeitwa Kohathi. Na sehemu yao walikuwa ni wazawa wa Haruni, ambaye ni mjukuu wa Kohathi.

miji kumi na tatu....miji kumi

Hii ni hesabu ya miji

Nusu kabila

Nusu ya kabila kwasababu nusu nyingine ilikuwa imepokea urithi wake kabla ya kuvuka Mto Yordani.

Joshua 21:6

Gershoni

Gershoni alikuwa ni mmoja wa wana wa Lawi

Upigaji wa kura

Hii ni njia ya kuchagua ambayo ilikuwa ya kubahatisha yaani bila mpango maalumu ili kuondoa utashi wa viongozi, mara kwa mara ilifanywa kwa wazo kuwa Mungu ataamua matokeo

Merari

Merari alikuwa ni mmoja kati ya wana wa Lawi

Joshua 21:8

Yahweh alivyokuwa ameagiza kwa mkono wa Musa

Kirai "kwa mkono wa" kina maana kwamba Yahweh alimtumia Musa kama chombo ili kuleta agizo lake.

koo za Wakohathi

Makuhani katika kundi hili walikuwa ni wazawa wa mwana wa Lawi aliyeitwa Kohathi. Sehemu yao nyingine walikuwa ni wazawa wa Haruni, ambaye ni mjukuu wa Kohathi.

Upigaji wa kura

Hii ni njia ya kuchagua ambayo ilikuwa ya kubahatisha yaani bila mpango maalumu ili kuondoa utashi wa viongozi, mara kwa mara ilifanywa kwa wazo kuwa Mungu ataamua matokeo

Joshua 21:11

Arba alikuwa ni baba wa Anaki

Haya ni maelezo ya nyuma juu ya jina la mtu aliyeuanzisha mji wa Kiriathi Arba.

Anaki

Hili ni jina la mwanaume

Nchi ya milima

Hii ni sehemu ya nchi ambayo kiuasilia imeinuka, ni ndogo kuliko mlima

Maeneo ya malishi

Hii ni sehemu iliyo na majani mengi au mimea inayofaa kwa ajili ya kulishia mifugo au wanyama

Mashamba ya mji

Maeneo ya nchi yaliyo wazi, mara nyingine huwa imepandwa mazao ambayo ni mali au yameuzunguka mji.

Vijiji

hizi ni jamii ndogo, mara nyingi ni ndogo kuliko mji

Joshua 21:13

Libna...Yatiri...Eshetmoa...Holoni...Debiri...Aini...Yutta

haya ni majina ya miji

miji tisa...makabila mawili

hesabu ya miji na makabila katika kifungu

Joshua 21:17

Kutoka katika kabila la Benyamini walipewa Gibea pamoja na maeneo yake ya malisho, na Geba

hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Kabila la Benyamini lilipewa Gibea."

Geba...Anathothi...Almoni

haya ni majina ya miji

miji kumi na tatu

"miji 13"

Joshua 21:20

familia ya Kohathi

Makuhani katika kundi hili walikuwa ni wazawa wa mwana wa Lawi aliyeitwa Kohathi. Sehemu yao nyingine walikuwa ni wazawa wa Haruni, ambaye ni mjukuu wa Kohathi.

walipewa miji

Hii inaweza kuelezwa muundo tendaji: "Walipokea miji"

upigaji wa kura

Hii ni njia ya kuchagua ambayo ilikuwa ya kubahatisha yaani bila mpango maalumu ili kuondoa utashi wa viongozi, mara kwa mara ilifanywa kwa wazo kuwa Mungu ataamua matokeo

Gezeri...Kibzaimu...Bethi Horoni

haya ni majina ya miji

miji minne kwa ujumla

Hii inarejelea orodha kwa hesaby yake kwa jumla.

Joshua 21:23

Kutoka katika kabila la Dani, ukoo wa Kohathi ulipewa Elteke

Hii inaeweza kuelezwa kwa kutumia muundo tendaji. "Kabila la Dani waliwapa ukoo wa Kohathi eneo la Elteke.

ukoo wa Kohathhi

Makuhani katika kundi hili walikuwa ni wazawa wa mwana wa Lawi aliyeitwa Kohathi. Sehemu yao nyingine walikuwa ni wazawa wa Haruni, ambaye ni mjukuu wa Kohathi.

Elteke...Gibethoni..Aijaloni...Gathrimoni

Haya ni majinia ya miji

Joshua 21:25

Kutoka katika nusu ya kabila la Manase, ukoo wa Kohathi walipewa miji miwili - Taanak

Hii inaweza kuelezwa kwa kauli tenda. "Nusu ya kabila la Manesa waliwapa ukoo wa Kohathi mji wa Taahaki."

Taanaki ...Gathirimmoni

Haya ni majina ya miji

miji miwili...miji kumi kwa ujumla

Hesabu ya miji iliyoorodhoshwa

ukoo wa Kohathi... koo za Wakolathi

Makuhani katika kundi hili walikuwa ni wazawa wa mwana wa Lawi aliyeitwa Kohathi. Sehemu yao nyingine walikuwa ni wazawa wa Haruni, ambaye ni mjukuu wa Kohathi.

Joshua 21:27

Kutoka katika nusu ya kabila la Manase, jamaa za Gershoni, ambazo hizi zilikuwa ni koo zingine za Walawi, zilipewa Golan

Maelezo haya yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Nusu ya kabila la Manase, koo zingine za walawi, walipokea kutoka kwa nusu ya kabila la Manase mji wa Golani."

Golani...Beeshitera

Majina ya miji

aliyeua mtu bila kukusudia

Hii na kifo kilichotokana na tendo la ambaye hakukusudia kumdhuru mtu.

miji miwili

hesabu ya miji

Joshua 21:28

Koo za Gershoni zilipewa pia miji minne kutoka kwa kabila la Isakari - Kishoni

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Koo za Gershoni walipokea pia Kishoni"

Kishoni....Daberathi...Yarmuthi....Enganimu...Mishali...Abdoni...helkathi...Rehobu

Haya ni majina ya miji

Kutoka katika kabila la Asheri, walipewa miji minne kwa ujumla - Mishali

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tenda. "Walipokea kutoka kabila la Asheri mji wa Mishali."

miji minne kwa ujumla

Hii inarejelea hesabu ya miji iliyoorodheshwa

Joshua 21:32

Kutoka kwa kabila la Nafutali, nasaba za Gershoni walipewa miji mitatu kwa ujumla - Kedeshi

Muundo tendaji unaweza kutumika pia. "Koo za Gershoni zilipokea Kadeshi kutoka kwa kabila la Nafutali"

Gershoni

Hili ni jina la mtu

Hamothidori...Kartani

Haya ni majina ya miji

miji kumi na mitatu kwa ujumla

"miji 13 kwa ujumla wake"

Joshua 21:34

Na kwa Walawi waliosalia, koo za Merari waliokuwa wamepewa kutoka katika kabila la Zabuloni: Yokneamu

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji: "Walawi waliobaki - koo za Merari - walipokea Yokneamu kutoka katika kabila la Zabuloni

Merari

Jina la mtu

Yokneamu ..Karta..Dimna ....Nahalali

Majina ya miji

miji minne kwa ujumla

Miji inarejelewa kwa ujumla katika hesabu yake.

Joshua 21:36

Kwa mbari za Merari walipewa miji minne kutoka katika kabila la Rubeni: Bezeri

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Koo za Merari zilipata Bezeri kutoka katika kabila la Rubeni."

miji minne

Hii inarejelea jumla ya hesabu ya miji

Bezeri...Yahazi...Kedemothi...Mefaathi...Ramothi

majina ya miji

Kutoka katika kabila la Gadi walipewa miji ya Ramothi

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. " Walipata mji wa Ramothi kutoka kwa kabila la Gadi."

Mahanaimu

Hili ni jina la mji

Joshua 21:39

Koo za Merari zilipewa pia Heshiboni

Maelezo haya yaweza kuelezwa kwa muundo tandaji. " Koo za Merari zilipata pia mji wa Heshiboni"

Heshiboni...Yazeri

haya ni majina ya miji

miji kumi na miwili kwa ujumla

"miji 12 jumla yake"

miji kumi na miwili walipewa wao kwa kupiga kura.

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Walipata miji kumi na miwili kwa kupiga kura."

kupiga kura

Hii ni njia ya kuchagua ambayo ilikuwa ya kubahatisha yaani bila mpango maalumu ili kuondoa utashi wa viongozi, mara kwa mara ilifanywa kwa wazo kuwa Mungu ataamua matokeo

Joshua 21:41

Miji waliyopewa Walawi kutoka katikati ya nchi

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Walawi walipata miji yao katika sehemu ya katikati ya nchi"

miji Arobaini na minane

"miji 48"

Joshua 21:43

aliwaapia

"alitoa kiapo"

Hakuna hata adui mmoja atakayeweza kuwashinda

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Walimshinda kila mmoja miongoni mwa adui zao."

Yawhew aliwatia maadui wao wote mikononi mwao.

hapa kirai "mikononi mwao" ina maana "ndani ya mamlaka yao"

Hakuna hata kitu kimoja miongoni kwa ahadi nzuri ambazo Yahweh alizisema kwa nyumba ya Israeli ambazo hazikutimia. Ahadi zote zilitimia

sentensi imeelezwa kwa kukanusha ili kutia nguvu maelezo yake. "Kila ahadi njema ambayo Yahweh alikuwa ameisema kwa nyumba ya Israeli ilikuwa kweli."

Joshua 22

Joshua 22:1

Warubeni

watu wa kabila la Yuda

Wagadi

Watu wa kabila la Gadi

Mmeitii sauti yangu

mahali hapa "sauti yangu" ina maana ya vitu ambavyo Yoshua alikuwa amevisema. "mlitii kila kitu nilichosema."

Bado hamjawaacha ndugu zenu

Hii inaweza kusemwa kwa namna isiyo ya kukanusha. "Mmebakia pamoja na ndugu zetu."

Joshua 22:4

kutembea katika njia zake

Mtu anayemtii Yahweh anasemwa kana kwamba alikuwa anatembea katika njia au barabara za Yahweh. "kutii kila kitu anachokisema"

kwa moyo wenu wote na kwa roho zenu zote.

Maneno "moyo" na "roho" hapa yametumika kurejelea mtu mzima. "kwa vyote unavyovifikiria na kuvihisi" au "kwa utu wako mzima"

Joshua 22:7

Yordani

Jina la Mto Yordani

chuma

Metali ngumu, imara na ya sumaku

nyara

jeshi lililoshinda huchukua kila kitu chenye thamani kutoka kwa watu waliowashinda.

Joshua 22:9

amri za Yahweh, kwa mkono wa Musa.

Kirai "kwa mkono wa" kina maana ya kwamba Yahweh alimtumia Musa kama wakala kufikisha agizo lake. "Amri ambayo Yahweh alimwambia Musa awapeni ninyi."

Joshua 22:10

Yordani

Huu ni ufupisho wa Mto Yordani

mbele ya nchi ya Kanaani

Makabila ya Israeli walioishi ng'ambo ya Mto Yordani wangeingia Kanaani kwa kupitia sehemu ambayo walijenga madhabahu. Hii sehemu inasemwa kana kwamba ilikuwa mbele ya au kwenye lango la kuingia Kanaani ambapo makabila mengine yalikuwa yanaishi.

Gelilothi

Jina la mji

Joshua 22:12

vita

hali ya mapigano au ugomvi wa silaha baina ya mataifa mawili au makundi ya watu.

Joshua 22:13

Eliezari

Jina la mtu

Joshua 22:15

Kusanyiko lote la Yahweh linasema

Watu wote wa Israeli wanasemwa kwa pamoja kwa umoja kana kwamba ni mtu mmoja. "Watu wengi wote wa Israeli wanauliza"

Joshua 22:17

Je dhambi zetu huko Peori hazikututosha?

Swali hili hutia mkazo juu ya dhambi zao za awali. Hii inaweza kuandikwa kwa maelezo haya. "Tumeshatenda dhambi huko Peori."

Bado hata sasa hatujajitakasa wenyewe kwa dhambi hiyo

sentensi hii inaweza kuelezeka vizuri kwa kauli ya kukubali. Bado tunahangaika na hatia za dhambi ile.

Je, nanyi leo pia mwageuka na kuacha kumfuata Yahweh?

Swali hili limetumika kwa ajili ya kuwakemea watu kwa ajili ya dhambi yao. Hii pia yaweza kuandikwa kama maelezo. "Hamtakiwi kugeuka na kuacha kumfuata Yahweh leo!"

Joshua 22:19

Akani...Zera

majina ya wanaume

Je hakuwa Akani mwana wa Zera aliyeivunja imani kwa vitu vile ambavyo vilikuwa vimetunzwa kwa ajili ya Mungu? Na je ghadhabu ya Mungu haikushuka kwa watu wote wa Israeli?

Maswali haya yametumika kuwakumbusha watu juu ya hukumu kwa ajli ya dhambi zilizopita. Maswali haya yanaweza yakaandikwa kama maelezo. "Akani mwana wa Zera, alitenda dhambi kwa kuchukua vitu vilivyokuwa vimetunzwa kwa ajili ya Mungu. Na kwasababu ya hiyo Mungu aliwaadhibu watu wote wa Israeli."

Joshua 22:21

Kama ilikuwa ni katika uasi..... basi Yahweh na atuadhibu.

Makabila matatu yanafanya kauli mbili zenye nadharia tete zinazosisitiza kuwa haikuwa kweli. Hawakujenga madhabahu ili kumwabudu mungu mwingine.

Joshua 22:24

Maelezo ya jumla

Makabila ya Rubeni, Gadi na nusu ya Manase wanatoa majibu yao sasa.

watoto wenu wanaweza kuwaambia watoto wetu.....Mungu wa Israeli?

Haya ni mashitaka ya kinadharia ambayo makabila haya matatu yanadhani kuwa watoto wa makabila mengine wangeweza kufanya kwa wakati ujao.

Mna nini ninyi na Yahweh, Mungu wa Israeli?

Makabila matatu yanatumia swali lisilohitaji majibu ili kutilia mkazo juu ya hali ambayo walikuwa wakiiepuka. Swali hili laweza kuandikwa kama maelezo. "Hamna kitu cha kufanya na Yahweh, Mungu wa Israeli."

Joshua 22:25

Maelezo ya jumla

Makabila ya Rubeni, Gadi, na nusu ya Manase yanaendelea kutoa majibu yao

Kwa kuwa Yahweh ameifanya Yordani....hamna kitu chochote naYahweh

Huu ni mwendelezo wa mashitaka ya kinadharia ambayo makabila yale matatu yanadhani kuwa watoto wa makabila mengine wangeweza kufanya kwa wakati ujao.

Yordani

Huu ni ufupisho wa Mto Yordani

watoto wenu wanaweza kuwafanya watoto wetu waacha kumwabudu Yahweh.

Makabila haya matatu yalijenga madhabahu ili kuepuka hali inayodhania isije ikatokea wakati ujao.

Joshua 22:26

Maelezo ya jumla

Makabila ya Rubeni, Gadi na nusu ya Manase wanatoa majibu yao sasa.

iwe ni ushahidi kati yetu na ninyi

Madhabahu inazungumzwa kana kwamba ilikuwa ni ushahidi ambao ungeweza kushuhudia haki kwa makabila matatu.

ili kwamba watoto wenu wasiweze kuwaambia watoto wetu katika siku zijazo kuwa, "Hamna sehemu katika Yahweh."'

Hii ni hali nadharia inayodhaniwa ambayo makabila matatu hayakutaka itokee.

ili kwamba watoto wenu wasiweze kuwaambia watoto wetu katika siku zijazo kuwa, "Hamna sehemu katika Yahweh."'

"hakuna sehemu" au " hamna urithi"

Joshua 22:28

Maelezo ya jumla

Makabila ya Rubeni, Gadi na nusu ya kabila la Manase wanamalizia kujibu sasa

'kama hili litasemwa....ushahidi kati yetu ninyi.

Makabila matatu yanaelezea uwezekano wa jibu lao kwa shutuma ambazo zinaweza kutokea au zisitokee hapo baadaye.

Na iwe mbali nasi kwamba tunataka kugeuka kinyume na Yahweh,

Nafasi isiyowezekana ya kuasi inasemwa kana kwamba ni kitu kilicho mbali sana kutoka kwao. "Hakika tusingeasi"

kuacha kumfuata yeye

kuacha kumfuata Yahweh kunasemwa kana kwamba walikuwa wanageukia mbali na kumwacha.

Joshua 22:30

waliposikia maneno

Hapa "maneno"yanarejelea juu ya ujumbe ambao uliundwa kwa maneno. "walisikia ujumbe"

yalikuwa ni mazuri machoni pao

Hapa maneno "machoni pao" inamaanisha "katika mawazo yao"

hamjatenda uvunjaji wa imani kinyume naye

"kuvunja agano lako kwake"

mmewaokoa watu wa Israeli kutoka katika mkono wa Yahweh.

Mahali hapa kirai "mkono wa Yahweh" inarejelea juu ya hukumu. Kitendo cha kulinda watu kinasemwa kama ni kuwaokoa kutoka katika mkono wake.

Joshua 22:32

Taarifa yao ilikuwa nzuri katika macho ya watu

Mahali hapa maneno "nzuri katika macho" ina maana ya "kupokelewa" "Watu waliipokea taarifa ya viongozi"

kuiharibu nchi

"kuharibu kila kitu katika nchi."

Joshua 22:34

kwa kuwa walisema

Hii inarejelea kwa Warubeni na Wagadi

Ni ushahidi miongoni mwetu

Madhabahu inasemwa kana kwamba alikuwa ni shahidi ambaye angeshuhudia kwa ajili ya makabila matatu.

Joshua 23

Joshua 23:1

mzee sana

aliishi miaka mingi

Joshua 23:4

Yordani

Kifupisho cha Mto Yordani

Upande wa magharibi

Hii inaonesha mwelekeo wa machweo ya jua.

Joshua 23:6

msikengeuke upande wa kulia wala upande wa kushoto

Kitendo cha kutotiii maagizo ya sheria za Musa kinasemwa kana kwamba ni kugeuka upande wa kulia au upande wa kushoto mbali na njia sahihi.

msichanganyikane

Maana zinazokubalika 1)kuwa na urafiki wa karibu nao 2) kuoana nao

msiyataje

kuyasema

miungu yao

Hii inarejelea juu ya miungu ya mataifa yaliyosalia.

kumshika sana Yahweh

"kumshikilia Yahweh kwa nguvu" Kumwamini Yahweh kunasemwa kana kwamba ni kumshikilia kwa nguvu.

hadi leo

"mpaka muda wa sasa"

Joshua 23:9

kusimama mbele yenu

Mahali hapa neno "kusimama" linawakilisha kujiweka imara kwa kusimama juu ya ardhi katika vita. Neno "yenu" linalejelea taifa zima la Israeli.

mmoja

namba moja

elfu

"1,000"

Joshua 23:12

kushikamana na watu walioalia wa mataifa haya walioba

Kitendo cha kubali imani za mataifa haya kunasemwa kana kwamba ni kuwashikilia kwa nguvu. "kubali imani za watu walisalia za mataifa haya."

kitanzi na mtego

Maneno haya "kitanzi" na "mtego" kimsingi yanamaanisha kitu kile kile. kwa pamoja yanaongelea juu ya mataifa mengine kana kwamba yalikuwa ni mitego hatari kwa waisraeli kwa kusababisha matatizo.

viboko migongoni mwenu na miiba machoni mwenu

Virai hivi vinaongelea juu ya matatizo ambayo yataletwa na mataifa haya juu ya Israeli kana kwamba vilikuwa ni viboko na miiba kwao.

Joshua 23:14

Na sasa ninaenda katika njia ya dunia yote

Yoshua anatumia neno la upole kurejelea juu ya kifo chake. "Ninakwenda kufa"

mnajua kwa moyo na roho zenu zote

Mahali hapa maneno "moyo" na "roho" yana maana sawa. Kwa pamoja yanatia mkazo juu ya ufahamu wa ndani wa mtu binafsi.

Hakuna hata moja lililoshindikana

Maneno haya yanatia mkazo kwamba ahadi zote za Yahweh zimetimia. Hii pia yaweza kuelezwa kawa kauli kubalifu. "kila neno lilitimia"

Joshua 23:16

Atafanya hivi

Hii inarejelea juu ya hukumu iliyotishiwa katika mstari uliotangulia.

kuiabudu miungu mingine na kuiinamia

Virai hivi viwili kimsingi vinazungumzia juu ya jambo moja lile lile. Kirai cha pili kinaelezea jinsi watu "wanavyoabudu miungu mingine"

ndipo hasira ya Yahweh itawaka kinyume nanyi

"kuwaka"ni lugha ya picha kuonesha mwanzo wa hasira ya Yahweh, kama moto, inawashwa au inaanzishwa au inaanza kuwaka kiurahisi kama kwenye majani makavu au vijiti vidogo vidogo. "Yahweh ataanza kuwa na hasira nanyi"

Joshua 24

Joshua 24:1

Kisha Yoshua aliyakusanya pamoja makabila yote ya Israeli

Kitendo cha Yoshua kuyaalika makabila kinazungumzwa kana kwamba ni kuyakusanya kwa pamoja katika kikapu. "Yoshua aliyaomba makabila yote ya israeli yakutane pamoja naye."

wakajihudhurisha mbele

"walikuja na kusimama mbele ya" au "kuja mbele"

miaka mingi iliyopita

miaka mingi ya nyuma

Hiki ndicho

Yoshua anaanza kwa kunukuru kile Yahweh alikuwa amekisema hapo mwanzo. Nukuu inaendelea mpaka mstari wa 13.

Tera...Nahori

Haya ni majina ya wanaume

Joshua 24:3

Maelezo ya jumla

Yoshua anaendelea kunukuu kile ambacho Yahweh alikisema katika kujishughulisha kwake na watu wake.

Seiri

Jina la sehemu au mahali

Walishuka kwenda

Misri ilikuwa ni sehemu ya chini katika mwinuko wa nchi ya Kanaani

Joshua 24:5

Maelezo ya jumla

Yoshua anaendelea kunukuu kile ambacho Yahweh alikisema katika kujishughulisha kwake na watu wake

niliwatoa ninyi...niliwatoa baba zenu nje

Yahweh anaendelea kuelezea katika virai hivi viwili ambavyo vinawarejelea waisraeli wote, kwa wakati uliopita na wa sasa.

Joshua 24:7

Maelezo ya jumla

Yoshua anaendelea kunukuu kile ambacho Yahweh alikisema katika kujishughulisha kwake na watu wake

Baba zenu...yenu

Yahweh anaendelea kuelezea katika virai hivi viwili ambavyo vinawarejelea waisraeli wote, kwa wakati uliopita na wa sasa

bahari

hapa inarejelewa bahari ya mitende

jangwaani

sehemu isiyokaliwa na watu, kame,

Joshua 24:8

Maelezo ya jumla

Yoshua anaendelea kunukuu kile ambacho Yahweh alikisema katika kujishughulisha kwake na watu wake

nanyi

Neno "nanyi" ni wingi katika hotuba hii ikirejelea taifa lote la Israeli.

Yordani

Ni ufupisho wa Mto wa Yordani

niliwatia katika mkono wenu

Hapa neno "mkono" linarejelea nguvu, uwezo au mamlaka. "kuwawezesha ninyi ili kuwashinda"

Joshua 24:9

Maelezo ya jumla

Yoshua anaendelea kunukuu kile ambacho Yahweh alikisema katika kujishughulisha kwake na watu wake

Balaki...Zipori

majina ya wanaume

ninyi

Neno hili "ninyi" limetumika katika wingi kurejelea taifa lote la Israeli.

niliwaokoa na mkono wake

Hapa neno "mkono" linarejelea nguvu, uwezo au mamlaka. "kuwawezesha ninyi ili kuwashinda"

Joshua 24:11

Maelezo ya jumla

Yoshua anaendelea kunukuu kile ambacho Yahweh alikisema katika kujishughulisha kwake na watu wake

Nanyi

Neno hili "nanyi" limetumika katika wingi kurejelea taifa lote la Israeli.

Yordani

hiki ni kifupisho cha Mto Yordani

manyigu

ni wadudu wadogo wanaopaa kwa kasi wanaoishi katika kundi kubwa la wadudu.

Joshua 24:13

Maelezo ya jumla

Yoshua anahitimisha kunukuru kile ambacho Yahweh alikuwa amekisema katika kushughulika na watu wake.

Joshua 24:14

Na kama inaonekana kuwa ni vibaya machoni penu

Hapa maneno "machoni penu" ni lugha mbili za picha zimetumika, inarejelea kwanza kwa macho yao, au inahusishwa na hamu/tamaa yao.

nyumba yangu

Hapa inarejelea familia iliyoishi katika nyumba yake.

Joshua 24:16

sisi na baba zetu ..sisi

Watu wanaongea kana kwamba walikuwa pamoja na baba zao kwa wakati huo, na kuongea maneno haya "sis" na "baba zetu"

nyumba ya utumwa

Mahali hapa neno "nyumba" ni lugha ya nahau kurejelea sehemu/mahali pa utumwa wao. "sehemu ambapo sisi tulikuwa watumwa"

mataifa yote ambayo tulipita kati kati yake

"mataifa ambayo sisi tulipita katikati yake"

Joshua 24:19

watu

hii inawarejelea Waisraeli

Mungu mwenye nguvu

Mungu anataka watu wake kumwabudu Yeye peke yake

Atawaangamizeni

Hasira ya Yahweh inaongelewa kana kwamba ilikuwa ni moto ambao ungewateketeza.

Joshua 24:21

Watu

inawarejelea Waisraeli

geuzeni moyo wenu umwelekee Yahweh,

Kuamua kumtii Yahweh ni kitendo kinachosemwa kuwa ni sawa na kugeuza moyo wao kumwelekea Yeye. Mahali hapa, neno "moyo" linawakilisha mtu mzima. Na kwa hali hii, "moyo" liko katika wingi kurejelea Waisraeli kama kundi moja.

Joshua 24:24

Watu

inawarejelea Waisraeli

Tutaisikiliza sauti yake

Mahali hapa neno "kuisikiliza" lina maana ya kutii. "Tutatii kila kitu atakachotwambia kufanya"

Aliziweka maagizo na sheria

Kitendo cha kuweka sheria kinasemwa kana kwamba Yoshua aliweka kitu halisi mahali fulani.

kitabu cha sheria za Mungu

Hii inaonekana kuwa ni mwendelezao wa maandishiya Musa

kulisimamisha hapo

"kuliweka hapo"

Joshua 24:27

watu

Inawarejelea Waisraeli

jiwe hili litakuwa ushuhuda ....limeyasikia maneno yote

Jiwe ambalo Yoshua aliliweka linasemwa kana kwamba alikuwa ni mtu ambaye alisikia kile kilichosemwa na angekuwa na uwezo wa kushuhudia juu ya kile kilichosemwa.

hamtakiwi

"kama mtafanya"

Joshua 24:29

miaka 110

"miaka mia moja na kumi"

Timnathi Sera...Mlima Gaashi

haya ni majina ya sehemu/mahali

Joshua 24:31

Siku zote za Maisha ya Yoshua

Lugha hii imetumika kuonesha maisha yote ya Yoshua.

walidumu pamoja na Yoshua

"waliishi muda mrefu zaidi ya Yoshua"

Joshua 24:32

Mifupa ya Yusufu ambayo watu wa Israeli waliileta kutoka Misri, waliizika huko shekemu

Mpangilio wa sentensi hii unaweza kubadilishwa hasa sehemu yake ya mwanzo ili kuleta msaada zaidi. "Watu wa Israeli walileta mifupa ya Yusufu kutoka Misri na kuizika huko Shekemu"

vipande mia moja

"vipande 100"

Eliazeri

Jina la mwanaume

Gibea

Hili ni jina la sehemu/mahali

Judges 1

Judges 1:1

Sentensi unganishi

Kitabu cha Waamuzi kinaendeleza simulizi ya Yoshua na pia ni mwanzo wa simulizi nyingine mpya.

atawashambulia Wakanaani kwa ajili yetu,

Neno "yetu" linamaanisha wana wa Israeli

Yuda atawashambulia

Hapa "Yuda" linawakilisha watu wa kabila la Yuda. Mungu anawaamuru watu hawa kushambulia kwanza. "Watu wa Yuda watashambulia kwanza"

Tazama

"Angalia" au "kweli". Hii inaongeza msisitizo wa kile kinachofuata.

Nchi hii

Hii inamaanisha nchi ambayo Wakanaani waliishi. "nchi ya Wakanaani"

Ndugu zao

"waisraeli wenzao" au "ndugu zao"

Njooni pamoja nasi

Watu wa kabila la Yuda na Simeoni waliweka kambi pamoja na Waisraeli katika bonde la mto Yordani. Yuda alipewa nchi ambayo ipo kwenye vilima juu ya bonde. Lugha zingine hazijaelezea kama watu walikwenda juu au chini. "njooni pamoja nasi" au "twendeni pamoja"

ambalo tulipewa... ambali mlipewa

"Ambalo Bwana alitupa sisi... ambalo Bwana aliwapa ninyi"

Tutakwenda pamoja nanyi

"sisi pia tutakwenda pamoja nanyi" au "kwa namna ile ile tutakwenda pamoja nanyi"

Judges 1:4

Watu wa Yuda wakavamia

Inamaanisha kwamba watu wa Simoni walivamiwa na watu wa Yuda.

Wakawaua watu elfu kumi

"waliwaua watu takribani 10,000" au "waliua idadi kubwa ya watu"

Hao

"askari Wakanaani na Waperizi" au "maadui"

Bezeki

Hili ni eneo la milima ya Kanaani

Adoni Bezeki

Alikuwa kiongozi wa jeshi la Wakanaani na Waperizi

Wakapigana naye

"naye" inamuelezea Adoni Bezeki na jeshi lake. "walipigana naye pamoja na jeshi lake"

Judges 1:6

Wakamfuata

"wakamkimbiza"

Wafalme sabini

"Wafalme 70"

walikusanya chakula chao chini ya meza yangu

"walikula vipande vya chakula chili ya meza yangu." Aliwalazimisha hawa wafalme kula vipande vya chakula inaonesha namna gani Adoni Bezeki alivyowanyanyasa hawa wafalme.

ambao na vidole gumba vyako na vidole vikubwa vilikatwa

"niliwaambia watu wangu wavikate vidole gumba vyao na vidole vikubwa"

Judges 1:8

jiji la Yerusalemu na kulichukua

Hapa "jiji" lina maanisha watu. "watu wanaoishi Yerusalemu na kuwashinda"

Walishambulia

Walishambulia jiji linaliwakilisha watu wa mji. "Walishambulia watu wa jiji"

kwa makali ya upanga

Hapa "Upanga" inamaanisha upanga au silaha nyingine inayotumiwa na askari vitani. "na upanga wao" au "na silaha zao"

watu wa Yuda walikwenda chini kupigana

Ilikuwa kawaida kutumia neno chini ikiwa ina maanisha kusafiri toka Yerusalemu. "Watu wa Yuda walikwenda kupigana"

Negebu

Kusini mwa jangwa la Yuda

Milima

vilima vilivyo chini ya mlima.

jina la Hebroni hapo awali ilikuwa Kiriath-arba

Hii ni taarifa. baadhi ya watu ambao walisoma kitabu hiki mwanzoni yamkini walisikia juu ya Kiriath-arba lakini hawakufahamu kuwa ilikuwa ni mji wa Hebroni.

Sheshai, Ahimani na Talmai

Haya ni majina ya viongozi watatu wa Kikanaani wa Hebroni. Kila kiongozi anawakilisha jeshi lake.

Judges 1:11

Maelezo ya jumla

Tazama: tafsiri ya majina

jina la Debiri hapo awali ilikuwa Kiriath-seferi

Mwandishi aliandika hivi kwa kuwa yamkini wasomaji wake walifahamu juu ya mji wa Debiri. lakini wakati ambao Israeli walivamia palikuwa pakiitwa Kiriath-seferi.

Awali

"siku za nyuma" au "wakati wa nyuma"

Yeyote atakayeivamia Kiriath-seferi na kuichukua

"Kiriath-seferi" ina maanisha watu. Yeyote atakayeivamia na kuiteka Kiriath-seferi na kuchukua mji wao"

Aksa

Jina la binti wa Kalebu

Otinieli, mwana wa Kenazi

Haya ni majina ya wanaume

Judges 1:14

Akamsihi

"Aksa akamsihi Othnieli"

akampa nchi ... kwa kuwa umenipa nchi

Hii inaelezea kuwa Kalebu alimpa nchi aliyoiomba katika sura ya 14. Katika sura ya 15 anaomba sasa na chemichemi ya maji.

Nibariki

"Nepe neema" au "Nifanyie hivi"

Kwa kuwa umenipa nchi ya Negebu

Kalebu alimpa Aksa aolewe na Othnieli, hivyo aliishi pamoja na Othnieli katika mji waliouteka Negebu.

Judges 1:16

Mkwe wake na Musa

"mkwe" "baba yake na mke wa musa"

Mkeeni, mkwe alikwenda

"mkwe ambaye alikuwa ni moja ya watu wa Keeni, alikwenda"

walikwenda kutoka mji wa Mitende ... mpaka jangwa

"aliondoka kwenye mji wa mitende ... akaenda jangwani"

Mji wa mitende

Hili ni jina lingine la mji wa Yeriko

Arad

Hili ni jina la mji wa Kanaani

wana wa Simeoni ndugu zao

"ndugu" hii inamaanisha ndugu waliopo katika kabila lingine la Israeli.

Zefathi

Hili ni jina la mji wa Kanaani

Mji uliitwa Horma

Baada ya Israeli kuiharibu Zefathi, walibadilisha jina na kupaita Horma. Jina Horma lina maana ya "uharibifu kamili."

Judges 1:18

Yahweh alikuwa pamoja na watu wa Yuda

"alikuwa pamoja" ina maana ya kwamba Bwana aliwasaidia watu wa Yuda.

Bonde

eneo kubwa lisilo na miti

Judges 1:20

Hebroni alipewa Kalebu (kama Musa alivyosema)

"Musa alimkabidhi Hebroni kwa Kalebu"

wana watatu wa Anaki

Viongozi wa watu wa kundi wamezoea kumaanisha kundi zima. "wana watatu wa Anaki na watu wao"

Anaki

Hili ni jina la mtu. Uzao wake wana sifa ya kuwa warefu sana wa kimo.

Hata leo

"mpaka sasa" Hii inamaanisha wakati kitabu cha Waamuzi kilipokuwa kinaandikwa.

Judges 1:22

Nyumba ya Yusufu

Hapa "Nyumba" inamaanisha uzao. Manase na Efraimu walikuwa watoto wa Yusufu na "nyumba ya Yusufu" inaweza kuwa na maana ya uzao wa Manase na Efraimu. "uzao wa Manase na Efraimu"

kushambulia Betheli

"Betheli" inamaanisha watu wanaoishi Betheli.

peleleza

kupata taarifa kwa siri

jiji lililoitwa Luzu

Hii ni taarifa. watu wengine waliosoma kitabu hiki kwa mara ya kwanza yamkini walisikia kuhusu Luzu ila hawakufahamu kuwa ni sawa na mji ulioitwa Betheli.

Wapelelezi

Watu wanaopata taarifa kwa siri

Judges 1:25

Waliuteka mji

"mji" inamaanisha watu. " Waliwateka watu wa mji"

kwa makali ya upanga

Hapa "Upanga" inamaanisha upanga au silaha nyingine inayotumiwa na askari vitani. "na upanga wao" au "na silaha zao"

Waondoke

"toroka"

Luzu

Mji huu mpya ulianza katika nchi ya Wahiti.

ambalo jina lake hata leo.

"ambalo bado ni jina lake.

Judges 1:27

Bethsheani ...Taanaki ... Dori ... Ibleamu ... Megido

Haya ni majina ya miji

kwa sababu Wakanaani walikuwa wameamua kuishi katika nchi hiyo

"kwa sababu Wkanaani waliamua kwa dhati kuwa hawataiacha hiyo nchi"

Israeli ipokuwa na nguvu

"Israeli" inamaanisha watu. "Watu wa Israeli walipokuwa na nguvu"

waliwalazimisha Wakanaani wawatumikie kwa kazi ngumu

"Waliwalazimisha wakaanani wawafanyie kazi ngumu"

Judges 1:29

Efraimu hakuwafukuza

"Efraimu" ni watu au askari wa kabila la Efraimu.

Gezeri

Jina la mji katika Efraimu.

Judges 1:30

Zebuloni hakuwafukuza

"Zebuloni" ni watu au askari wa kabila la Zebuloni.

Kitroni ... Nahaloli

Haya ni majina ya mji katika nchi ya Kanaani.

lakini Zebuloni akawalazimisha

"Zebuloni" ni watu wa kabila la Zebuloni.

kazi ngumu

"kazi ngumu"

Judges 1:31

Asheri hakuwafukuza

"Asheri" linamaanisha watu au askari wa kabila la Asheri.

Aka ... Sidoni ...Alabu, Akzib, Helba, Afeka ... Rehobu.

Haya ni majina ya miji katika nchi ya Kanaani.

Judges 1:33

Bethshemeshi ... Bethanathi.

Hata ni majina ya miji

wenyeji wa Bethshemeshi na Bethanathi walilazimishwa kufanya kazi ngumu kwa Naphthali.

Hii inaweza kutafsiriwa kama "watu wa Naftali walilazimishwa na watu wa Bethshemeshi naa Bethanathi kuwafanyia kazi kama watumwa.

Judges 1:34

Maelezo ya jumla

Tazama; tafsiri ya majina

hawakuwaruhusu kuja bondeni

"aliwakataza kushuka bondeni"

bonde

eneo kubwa la ardhi lisilo na miti

Mlima wa Heresi

Hili ni jina la mlima mkubwa ambapo mji wa Aiyaloni ulijengwa.

Aiyaloni... Shaalbimu,

Haya ni majina ya miji

nguvu za kijeshi za nyumba ya Yusufu ziliwashinda

"kabila la watu wa uzao wa Yusufu waliweza kuwashinda kwa sababu walikuwa na jeshi lenye nguvu"

Nyumba ya Yusufu

Hapa "Nyumba" inamaanisha uzao. Manase na Efraimu walikuwa watoto wa Yusufu na "nyumba ya Yusufu" inaweza kuwa na maana ya uzao wa Manase na Efraimu. "uzao wa Manase na Efraimu"

kilima cha Akrabimu

Hiki kilikuwa njiani kusini mashariki na Bahari ya shamu. Pia inaitwa "njia ya nge"

Sela

Hili ni jina la mji

Judges 2

Judges 2:1

Malaika wa Bwana

yaweza kuwa na maana ya 1) "malaika anayemuwakilisha Bwana" au 2) "malaika anayemtumikia Bwana" au 3) yaweza kumaanisha Bwana mwenyewe, aliyeonekana kama malaika akiwa anazungumza na mtu.

akatoka Gilgali, akaenda Bokimu

"akaondoka Gilgali akaenda Bokimu"

Bokimu

Wana wa Irsaeli walipaita mahali hapa katika sura ya 2:5 baada ya malaika kuwakemea watu. "Bokimu" ina maana ya "kilio"

akasema

inaeleweka kuwa malaika wa Bwana alikuwa akizungumza na wana wa Israeli. "akasema na wana wa Israeli"

Nimekuleta kutoka Misri

"nimekutoa Misri"

Baba zako

"mababu zako"

kuvunja agano langu na wewe

"kushindwa kufanya yale niliyopaswa kufanya kwako"

Haukuisikiliza sauti yangu

"sauti" ina maanisha alichokisema Bwana. "haukusikiliza ammri zangu"

Ni nini hiki ulichokifanya?

Swali hili linaulizwa ili kuwafanya wana wa Israeli wagundue kuwa hawajamtii Mungu na watateseka kwa sababu hiyo. "Mmefanya jambo baya"

Judges 2:3

Maelezo ya jumla

Malaika wa Bwana anaendelea kuzungumza na wana wa Israeli.

Basi sasa nasema, "Sitawafukuza... miiba kwenu

Hii ni nukuu ndani ya nukuu. "Basi sasa nawaambia sitawafukuza ... miiba kwenu.'"

watakuwa miiba kwenu

Wakanaani wanaowasumbua Waisraeli wanazungumzwa kuwa Wakanaani watakuwa miiba kwa Waisraeli. "watawasababishia matatizo"

Miiba

Kipande cha mbao chenye ncha kali mpaka sentimeta 7 ambacho huchomoza pembeni ya mmea.

miungu yao itakuwa mtego kwa ajili yenu

Waisraeli kuabudu miungu ya Wakanaani ni sawa na miungu ya uongo inayofananishwa na mtego wa mwindaji unaowakamata wanyama na kusababisha madhara.

wakapiga kelele na kulia

"wakalia machozi mengi"

Judges 2:6

Sasa Yoshua

"Sasa" imetumika kama alama ya kituo toka kwenye simulizi. Hapa mwandishi anaanza kwa kuelezea uzao wa Israeli baada ya Yoshua kuasi na kuabudu miungu ya uongo na Bwana akawaadhibu, lakini atawatuma waamuzi kuja kuwaokoa.

Yoshua alipo ... alikufa akiwa na umri wa miaka 110

Matukio ya 1:1-2:5 yalitokea baada ya Yoshua kufa. Hapa inahesabu matukio yaliyotokea mwishoni mwa kitabu cha Yoshua.

mahali alipopewa

"Mahali alipopewa na Bwana"

wakati wa maisha

Ina maana ya wakati ambao mtu alikuwa hai. "wakati wa uhai"

Wazee

Inamaanisha watu waliosaidia kuingoza Israeli, walioshiriki katika mambo ya kijamii na kidini kama vile kutii amri ya Musa.

Walioendelea baada yake

Hii inamaanisha kuishi mda mrefu zaidi ya mtu mwingine. "Kuishi mda mrefu zaidi yake"

Nuni

Hili ni jina la mwanamume.

Judges 2:9

Aliyopewa

"Ambayo Mungu alimpa"

Timnath Heresi

Hili ni jina la eneo.

Mlima Gaash

Hili ni jina la mlima

Kizazi hicho chote kilikusanyika kwa baba zao

Sentensi "kilikusanyika kwa baba zao" ina maanisha kwamba watu wa kizazi kile walikufa, nafsi zao zikaenda sehemu ile ile ambayo mababu zao waliokufa kwanza walienda. Ni namna nzuri ya kusema walikufa.

Baba

Hapa ina maanisha mababu wa mtu au kikundi fulani cha watu.

Kukua

"kuongezeka umri" au "kuwa mzee"

Ambao hawakumjua Bwana

"hawakumjua" ina maanisha hawakumtambua Bwana au nguvu zake kama ambavyo kizazi kilichopita kilimtambua.

Judges 2:11

Yaliyo mabaya machoni mwa Bwana

"machoni mwa Bwana" inawakilisha kile ambacho Bwana alikifikiria.

Mabaali

Huu ni wingi wa Baali. Baali ni jina la mungu wa uongo.

Wakaondoka kwa Bwana

Waisraeli hawakutii tena anayosema Bwana hivyo wakawa wameondoka mbele ya Bwana.

Baba

"Mababu"

Wakaifuata miungu mingine

Waisraeli kuanza kuabudu miungu ya uongo wanafananishwa kama Waisraeli walioondoka na kuifuata miungu ya uongo.

Wakaisujudia

Hili ni tendo la kuabudu au kutoa heshima kwa mtu.

Wakamkasirisha Bwana

Wakasababisha Bwana akasirike"

Maashtoreti.

Huu ni wingi wa Ashtoreti, aliyeabudiwa kama mungu kwa namna nyingi.

Judges 2:14

Hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli

Hasira ya Bwana inaelezewa kama moto uwakao. "Bwana akakasirika juu ya wana wa Israeli"

akawapa washambuliaji walioiba mali zao kutoka kwao

"Akawaacha washambuliaji waibe mali zao"

Aliwauza kama watumwa waliofanyika kwa nguvu za maadui zao waliowazunguka, hivyo hawakuweza kujikinga dhidi ya adui zao

Bwana akaruhusu adui zao wawachukue Waisraeli kama watumwa, wakauzwa utumwani. "Aliwaruhusu adui zao kuwashinda na kuwachukua kama watumwa na hawakuweza kuishinda nguvu ya adui"

mkono wa Bwana ulikuwa dhidi yao kuwashinda

"Mkono" inawakilisha nguvu ya Bwana. "Bwana aliwasaidia adui zao kuwashinda"

walikuwa katika shida kali

"Waliteseka sana"

Judges 2:16

Ndipo Bwana akawainua waamuzi

Bwana aliwachagua watu kuwa waamuzi akawainua.

katika mikono ya wale

"mikono" ni nguvu. "Toka kwenye nguvu za adui zao"

Hawakuwasikiliza waamuzi wao

"hawakuwatii waamuzi wao"

wakajitoa wenyewe kama makahaba kwa miungu mingine na kuabudu

Watu kumsaliti Mungu na kuiabudu miungu mingine wanafananishwa na makahaba. "walimsaliti kwa kuiabudu miungu ya uongo"

Waligeuka upesi na kuiacha njia waliyoishi baba zao

Watu hawakufanya kama vile babu zao walivyomuabudu Bwana, waligeukia upande mwingine.

Baba zao

"mababu zao"

Judges 2:18

Bwana aliinua waamuzi.

Bwana alichagua watu kuwa waamuzi kwa njia ya kuwainua juu.

waamuzi kwa ajili yao ... kuwaokoa

"yao" ina maanisha Waisraeli.

mikono ya adui zao

"mkono" ina maanisha nguvu za adui za kuwaumiza Waisraeli.

siku zote muamuzi aliishi

"kwa muda muamuzi alioishi"

Huruma

Kuwa na huruma juu ya kitu fulani au mtu

walipougua

Huu ni mlio unatolewa na mtu anayeteseka, inatumika kuelezea maumivu ya Waisraeli.

Waligeuka

Watu hawakuendelea kumtii Bwana waligeuka.

Baba zao

"mababu zao"

Wakaenda kuifuata miungu mingine kuitumikia na kuiabudu

Waisraeli kuiabudu miungu mingine inafananishwa kama vile walitembea kuifuata miungu mingine. "Waliitumikia na kuabudu miungu mingine"

Walikataa kuacha matendo yao yote mabaya au njia zao za ukaidi.

"Walikataa kuacha kufanya mambo maovu na wakawa wakaidi."

Judges 2:20

Hasira ya Bwana iliwaka juu ya Israeli

Hasira ya Bwana inaelezewa kama moto uwakao.

Taifa hili limevunjika

"taifa" inawakilisha watu. "watu hawa wamevunjika" au "Waisraeli wamevunjika"

Baba

Hapa inamaanisha mababu wa mtu fulani au wa kundi fulani la watu.

Hawakuisikiliza sauti yangu

"sauti" inawakilisha yale aliyosema Bwana. "hawajatii niliyowaamuru" au "hawajanitii mimi"

Taifa lolote

"taifa" inawakilisha kundi la watu walioishi Kanaani kabla ya Waisraeli.

Watashika njia ya Bwana na kuifuata

Namna ambavyo Bwana anataka watu waishi inafananishwa kama vile wapo njiani. Watu kumtii Bwana ni sawa na kutembea katika njia zake.

Hakumruhusu Yoshua kuwashinda

"hakumuacha Yoshua kuwashinda"

Hakumruhusu Yoshua

Hapa "Yoshua" anawakilisha jeshi lake. Hakumruhusu Yoshua na jeshi lake.

Judges 3

Judges 3:1

Sasa Bwana

"sasa" inaonesha mwanzo wa simulizi.

Mataifa haya

Hili ni kundi la watu wanaozungumzwa katika 3:3.

ambaye hakushiriki vita yoyote huko Kanaani

Inaweza kuanza kama "ambaye hakupigana vita yoyote huko Kanaani.

Alifanya hivyo ili kuwafundisha vita kizazi kipya cha Waisraeli ambao hawakujua kabla

Msimuliaji anatoa taarifa kwanini Bwana aliwaacha baadhi ya watu Kanaani. "Bwana aliyaacha mataifa kati ya Israeli ili awafundishe vijana ambao hawakupigana vita"

Wafalme watano

Wafalme hawa watano wanawakilisha watu wao. "wafalme watano na watu wao"

Mlima Baali Hermoni

Huu ni mlima mrefu sana Israeli.

Hamathi

Hili ni jina la eneo kaskazini mwa mpaka wa Kanaani.

Judges 3:4

Mataifa haya yaliachwa

Inaweza kuanza kama "Bwana aliyaacha mataifa haya Kanaani" au "Bwana aliruhusu mataifa haya kuendelea kuishi Kanaani"

kama njia

"kama namna"

kama watazitii ... alizowapa babu zao

Maneno "wao" na "zao" yanawaelezea wana wa Israeli.

amri alizowapa

"amri ambazo Bwana aliwapa"

Judges 3:7

yaliyo mabaya machoni pa Bwana

"machoni mwa Bwana" inawakilisha kitu ambacho Bwana anakifikiria au kuwaza juu ya jambo fulani.

wakamsahau Bwana, Mungu wao

"kumsahau" ni fumbo lenyhe maana ya "waliacha kumtii"

hasira ya Bwana ikawaka

Bwana kuwa na hasira inafananishwa na kitu ambacho kinaweza kuwaka moto. "Bwana akakasirika sana"

akawauza mkononi mwa Kushan-rishathaimu

Akaruhusu wana wa Israeli kutekwa inazungumzwa kama vile Bwana amewauza kwa Kushan-rishathaimu. "Akaruhusu Kushan-rishathaimu na jeshi lake kuwashinda"

mkononi mwa Kushan-rishathaimu

"mkono" ina maanisha nguvu ya kutawala. pia Kushan-rishathaimu inawakilisha jeshi lake.

Kushan-rishathaimu

Hili ni jina la mwanaume.

Aram Naharaimu

Hili ni jina la nchi.

Judges 3:9

Bwana akamuinua mtu

Bwana akamchagua mtu kufanya kazi maalumu kwa ajili yake.

Othnieli ... Kenazi

Majina haya ni ya wanaume.

akamtia nguvu

Maneno haya yanamaanisha kwamba Bwana akamsaidia Othnieli kukuza sifa alizozitaka ili awe kiongozi bora.

akahukumu Israeli

"kuhukumu" inamaanisha kuwaongoza wana wa Israeli.

naye akatoka kwenda vitani

"naye" inamuelezea Othnieli ambaye anawakilisha jeshi la Israeli. "Othnieli na jeshi la Israeli wakatoka kwenda kupigana na jeshi la Kushan-rishathaimu"

Bwana akampa kuishinda Kush-rishataimu mfalme wa Aramu

"Kush-rishataimu" anawakilisha jeshi lake. "Bwana akalisaidia jeshi la Israeli kulishinda jeshi la Kush-rishataimu mfalme wa Aramu"

Mkono wa Othnieli

Hapa neno "mkono" limesimama badala ya jeshi. "Jeshi la Othnieli"

Nchi ilikuwa na amani

"nchi" imetumika kuelezea watu waishio ndani yake. "Watu waliishi kwa amani"

Miaka arobaini

"miaka 40"

Judges 3:12

yaliyo mabaya machoni pa Bwana

"machoni mwa Bwana" inawakilisha kitu ambacho Bwana anakifikiria au kuwaza juu ya jambo fulani

Bwana akampa Egloni mfalme wa Moabu nguvu

"Bwana akamfanya Elgoni mfalme wa Moabu kuwa na nguvu"

Egloni mfalme wa Moabu, kuwashinda Waisraeli

"Egloni mfalme wa Moabu" inawakilisha jeshi lake. "Egloni mfalme wa Moabu na askari wake wakavamia jeshi la Israeli"

Egloni

Hili ni jina la mfalme.

mji wa Mitende.

Hili ni jina lingine la mji wa Yeriko.

Miaka kumi na nane

"miaka 18"

Judges 3:15

walipomwomba Bwana

Hii inamaanisha walipaza sauti kwa nguvu kwa mtu aliye mbali. pia inaweza kumaanisha mtu anaomba msaada hasa kwa Mungu.

akamwinua mtu

Bwana akamchagua mtu kufanya kazi maalumu kwa ajili yake.

Ehudi ... Gera

Haya ni majina ya wanaume.

mtu shoto

shoto. Ehudi alikuwa na uwezo wa kutumia upanga kwa mkono wa kushoto.

Judges 3:16

dhiraa moja

Kama kuna ulazima wa kutumia njia za kisasa za kupima urefu, kuna njia mbili za kufanya hivyo. "urefu sentimeta 46" au "urefu zaidi ya mita moja na nusu"

aliufunga chini ya nguo zake juu ya mguu wake wa kulia

"aliufunga kwenye mguu wake wa kulia chini ya nguo"

mguu

"paja"

Egloni alikuwa mtu mnene sana

Hapa msimuliaji anatupa taarifa juu ya Elgoni.

Judges 3:19

alipofikia mahali ambapo sanamu za kuchonga zilitengenezwa karibu na Gilgali,

"Alipofika mahali karibu na Gigali sehemu ambapo sanamu za kuchongwa hutengenezwa"

katika chumba cha juu cha baridi

Hiki ni chumba cha juu kilichotumika kwa ajili ya kupumzika na chenye ubaridi hata wakati wa joto.

Mfalme akasimama kutoka katika kiti chake

Kusimama ni ishara ya kumheshimu Mungu wakati wa kusikiliza ujumbe wake.

Judges 3:21

nao ukatokea nyuma yake

"ncha ya upanga ikatokea nyuma yake"

hakuutoa

"hakuuvuta"

ukumbi

Hiki ni chumba cha nje chenye ukuta mdogo na kilichoezekwa.

Judges 3:24

Hakika atakuwa anajitoa mwenyewe

Hii ni hali ya kuzungumza kwa upole kuhusu mtu ambaye anataka kujisaidia.

hata walipoanza kuhisi kuwa walikuwa wakipuuza wajibu wao

Walisubiri mpaka wakaanza kuwa na wasiwasi kuwa kuna kitu hakipo sawa na ulikuwa wajibu wao kufungua mlango katika chumba binafsi cha mfalme wao.

walichukua ufunguo wakawafungua

"walichukua ufunguo na kufungua mlango"

Judges 3:26

Wakati watumishi wakisubiri ... Ehudi alikimbia

Hii inaeleza nini kilitokea kabla watumishi hawajafungua mlango wa chumba cha juu na kukuta mfalme amekufa. "Wakati watumishi walipokuwa wakisubiri nje ya chumba cha juu ... Ehudi alikimbia"

Seira.

Hili ni jina la mji.

Alipofika

"Alipofika Seira"

Judges 3:28

Maelezo ya jumla:

Ehudi anazungumza na watu wa Israeli huko Efraimu.

kwa kuwa Bwana atawashinda adui zenu

Bwana aliwasaidia Waisraeli kuwashinda adui zao kama vile Bwana ndiye shujaa anayepigana na kuwashinda adui zao.

wakakamata vivuko

"Wakamiliki vivuko"

Vivuko

Sehemu ya mto ambayo ni rahisi kupita kuwenda upande mwingine.

hawakuruhusu mtu yeyote kuvuka

"hawakuacha mtu yeyote avuke"

Watu elfu kumi

"watu 10,000"

Watu wenye uwezo

"watu wenye uwezo wa kupigana vizuri"

Moabu ilishindwa na nguvu ya Israeli

Hii inaweza kuanza "jeshi la Waisraeli liliwashinda Wamoabu"

Nguvu ya Israeli

Hapa "nguvu" inawakilisha jeshi la Israeli.

nchi ilikuwa na amani

Hapa "nchi" inawakilisha watu. "Waisraeli waliishi kwa amani"

Miaka themanini

"miaka 80"

Judges 3:31

Mwamuzi

Mungu alichagua mwamuzi kuwaongoza wana wa Israeli katika nyakati za shida baada ya kuingia katika nchi ya ahadi na kabla ya kuwa na wafalme. mara nyingi waamuzi waliwaokoa Waisraeli toka kwa maadui.

Shamgari

Ni jina la mwanaume.

Athani

Ni jina la mwanaume.

konzo

"kusogeza" au "kuongoza"

Pia aliwaokoa Israeli kutoka kwenye hatari.

"Hatari" inamaanisha maadui waliotaka kuwadhuru Waisraeli.

Judges 4

Judges 4:1

Ehudi

Hili ni jina la mwanaume.

yaliyo mabaya machoni pa Bwana.

"machoni mwa Bwana" inawakilisha kitu ambacho Bwana anakifikiria au kuwaza juu ya jambo fulani

Bwana akawatia mkononi mwa Yabini, mfalme wa Kanaani

Hapa "mkono" ina maanisha nguvu za Yabini juu ya Israeli.

Yabini ... Sisera

Haya ni majina ya wanaume

Hasori ... Harosheti

Haya ni majina ya miji au mahali.

magari ya chuma mia tisa

"magari ya chuma 900"

miaka ishirini

"miaka 20"

Judges 4:4

Sasa

hapa msimuliaji anatuelezea habari kuhusu Debora.

Debora

Hili ni jina la mwanamke.

Lapidothi

Hili ni jina la mwanaume.

Mwamuzi

Mungu alichagua mwamuzi kuwaongoza wana wa Israeli katika nyakati za shida baada ya kuingia katika nchi ya ahadi na kabla ya kuwa na wafalme. mara nyingi waamuzi waliwaokoa Waisraeli toka kwa maadui.

mtende wa Debora

Mti huu ulipewa jina la Debora.

Judges 4:6

Taarifa ya jumla

Mwandishi wa Waamuzi anaelezea watu, miji, milima na mito kwa majina yake.

Baraka ... Abinoamu

Haya ni majina ya wanaume.

mlima wa Tabori

Hili ni jina la mlima.

watu elfu kumi

"watu 10,000"

Mimi nitamfukuza

"Mimi" linamaanisha Mungu.

Nitamfukuza Sisera

Hapa "sisera" inawakilisha jeshi lake. "nitamfukuza Sisera na jeshi lake"

Kufukuza

Kuwatoa watu waondoke sehemu salama.

Sisera ... Yabini,

Haya ni majina ya wanaume.

Kishoni

Hili ni jina la mto.

Judges 4:8

Taarifa ya jumla:

Baraka anafanya majadiliano na Debora.

Baraka

Hili ni jina la mwanaume.

njia unayoienda haitakupa heshima

Maamuzi aliyoyafanya Baraka yanafananishwa kama njia aliyoichagua Baraka kusafiria. Pia "heshima" inazungumzwa kama mwisho wa safari.

kwa kuwa Bwana atamuuza Sisera mkononi mwa mwanamke

Hapa "mkono" imetumika kama nguvu za kumuua. "Kwa maana Bwana atasababisha mwanamke amshinde Sisera"

Sisera

Hili ni jina la mwanaume.

Debora

Hili ni jina la mwanaume.

Judges 4:10

Watu elfu kumi

"watu 10,000"

Judges 4:11

Sasa

hapa msimuliaji anatuelezea habari kuhusu Heberi.

Heberi ... Hobabu

Haya ni majina ya wanaume.

Mkeni

Huyu ni mmoja ya watu wa Keeni.

Mkwe wa Musa

"Baba yake na mke wa Musa"

Saanaimu

Hili ni jina la mji.

Judges 4:12

Walipomwambia Sisera

Hapa haijambainisha mtu moja kwa moja. "mtu alipomwambia Sisera"

Sisera

Hili ni jina la mwanaume.

Baraka ... Abinoamu ... mlima wa Tabori

Baraka na Abinoamu ni majina ya mwanaume. Na mlima wa Tabori ni jina la mlima.

Sisera akayaita magari yake yote

"magari" yanawakilisha askari wanaoendesha magari.

magari ya farasi mia tisa

"Magari ya farasi 900"

Haroshethi

Hili ni jina la mahali.

Mto Kishoni.

Hili ni jinala mto.

Judges 4:14

Bwana amekupa ushindi

Debora ana uhakika na ushindi. anazungumza kama vile Baraka ameshapata ushindi. "Bwana atakupa ushindi"

Je! si Bwana anayekuongoza?

Debora anamuuliza hili Swali Baraka ili kumkumbusha kuwa wanapigana wakiwa upande wa Bwana. "Kumbuka Bwana anakuongoza"

Kumi elfu

"10,000"

Judges 4:15

Bwana alifanya jeshi la Sisera kuchanganyikiwa

"Bwana akamfanya Sisera ashindwe kufikiri vizuri" au Bwana akalifanya jeshi la Sisera kuchanganyikiwa"

magari yake yote

"magari" yanawakilisha askari wanaoendesha magari.

Baraka akayafuata

"Baraka" anawakilisha jeshi lake. Baraka na jeshi lake wakayafuata"

Haroshethi

Hili ni jina la mji.

jeshi lote la Sisera likauawa kwa upanga

Hapa neno "upanga" linawakilisha upanga au siliha nyingine ambayo askari hutumia vitani.

Judges 4:17

Sisera ... Yabini ... Hazori

Sisera na Yabini haya ni majina ya wanaume bali Hazori hili ni jina la mji.

akakimbia kwa miguu

Hii ina mana ya kuwa alikuwa anatembea kwa miguu na sio kutumia farasi.

Yaeli

Hili ni jinala mwanaume.

Heberi

Hili ni jina la mwanaume.

Mkeni

Huyu ni mmoja ya watu wa Keeni.

nyumba ya Heberi Mkeni

Hapa "nyumba" inawakilisha familia. "familia ya Heberi mkeni"

Akageuka kando

Hii inamaanisha kupumzika katika safari.

Bushuti

Ni shuka kubwa analojifunika mtu ili mwili upate joto wakati wa kulala, hutengenezwa kwa sufu au ngozi ya mnyama.

Judges 4:19

Akamwambia

"Sisera akamwambia Yaeli"

Judges 4:21

kigingi cha hema

Kipande cha mbao au chuma, kama sindano kubwa ambayo inachomekwa chini na kushikilia kona ya hema.

Nyundo

Kifaa kizito kinachotumika kugongea kigingi cha hema chini.

Usingizi mzito

Kama mtu aliye katika shimo kubwa hawezi kupanda juu, mtu aliye katika usingizi mzito haweze kuamka haraka.

kupenya

"ikatengeneza shimo"

Baraka alimfuata

"Baraka alimkimbilia" au "Baraka alimfuata kwa nyuma"

Judges 4:23

Mungu alimshinda Jabin, mfalme wa Kanaani, mbele ya watu wa Israeli

Mungu aliwafanya Waisraeli wamshinde Yabini pamoja na jeshi lake.

Uwezo

"Nguvu za jeshi"

wakamwangamiza yeye

"yeye" inamaanisha Yabini na jeshi lake. "Wakamwangamiza Yabini na jeshi lake"

Judges 5

Judges 5:1

Siku hiyo

Maana halisi ya sentensi hii yaweza kuwa "Siku hiyo Waisraeli walilishinda jeshi la Yabini"

Debora

Hili ni jina la mwanamke.

Baraka ... Abinoamu

Haya ni majina ya wanaume.

watu wanapojitolea kupigana vita

"watu walipokubali kupigana vitani"

Judges 5:3

Taarifa za jumla:

wimbo wa Debora na Baraka kwa kutumia ushairi unaendelea.

Sikiliza, ninyi wafalme! Sikiliza kwa makini, ninyi viongozi

Debora na Baraka wanazungumza na wafalme na viongozi kama vile wanawasikilizisha wimbo.

Ninyi wafalme ... ninyi viongozi

Hii inamaanisha wafalme na viongozi kwa ujumla, na sio viongozi au wafalme fulani.

wakati ulipotoka Seiri, ulipokwenda kutoka Edomu

Hii inarejea wakati ambao Waisraeli waliondoka Edomu na kuanza kuwateka watu wa Kanaani. Bwana aliwatia nguvu watu wake wakawashinda watu wa Kanaani.

Seiri

Huu ni mlima uliopo mpakani mwa Israeli na Edomu.

nchi ilitetemeka, na mbingu pia ilitetemeka; pia mawingu yalitoa maji.

Yaweza kuwa na maana ya 1) Hii ni lugha ya kishairi ambayo inasisitiza nguvu ya Bwana ambazo zina uwezo wa kusababisha tetemeko la ardhi au 2) watu wa Kanaani walianza kuogopa baada ya Waisraeli kutaka kuwavamia inafananishwa kama vile mbingu na nchi zinatetemeka.

Judges 5:5

Taarifa za jumla:

wimbo wa Debora na Baraka kwa kutumia ushairi unaendelea.

Milima inatetemeka

Imerejea tetemeko la ardhi ili kuonesha kuwa milima inatetemeka kwa sababu inamuogopa Bwana.

mbele ya uso wa Bwana

"uso" ina maanisha uwepo wa Bwana. "kwenye uwepo wa Bwana"

hata Mlima Sinai ukatetemeka

Musa na Waisraeli walipokuwa mlima Sinai ulitetemeka. "Hapo zamani hata mlima Sinai ulitetemeka"

Katika siku za

Hapa "siku" inawakilisha muda mrefu uliopita.

Shamgari ... Anathi ... Jael

Haya ni majina ya watu.

Mwana wa Anathi

Baba yake na Shamgari anatajwa ili kusaidia kumtambua Shamgari.

barabara kuu ziliachwa

"Watu waliacha kutumia barabara kuu kwa sababu waliwaogopa maadaui wa Israeli.

njia za upepo

Hizi ni njia ndogo ambazo watu wachache walizitumia.

Judges 5:7

mama alichukua amri katika Israeli

Hii inazungumzia juu ya uongozi wa Debora kama mama wa Israeli. "Aliwajali Waisraeli kama ambavyo mama anawajali watoto wake"

Walichagua miungu wapya

"Wana wa Israeli waliabudu miungo mipya"

kulikuwa na vita katika malango ya jiji

Neno "malango" linawakilisha mji mzima. "maadui waliwashambulia watu ndani ya miji ya Israeli"

hapakuwa na ngao au mikuki iliyoonekana kati ya watu elfu arobaini nchini Israeli.

Hii sentensi inaelezea ni kwa kiasi gani Waisraeli walikuwa na silaha chache.

elfu arobaini nchini Israeli

"40,000 nchini Israeli"

Judges 5:9

Moyo wangu unawaendea wakuu wa Israeli

"moyo" unawakilisha hisia za mtu. Debora anatoa shukrani kwa wakuu wa Israeli.

ninyi ambao hupanda punda weupe ... nanyi mnaotembea njiani.

Maelezo haya yanawaelezea matajiri na masikini, zote hizi zimetumika ili kumuelezea kila mtu.

mmeketi kwenye mazulia

Mazulia yalitumika kuweka kwenye mgongo wa punda ili kumfanya mtumiaji wa punda kuwa huru zaidi.

Judges 5:11

Taarifa ya jumla:

Wimbo wa Debora na Baraka unaendelea.

Sikiliza sauti za wale

"sauti" inawakilisha watu wakiimba.

wakashuka kwenye malango ya mji.

"malango" inawakilisha mji mzima. "wakarudi kwenye miji yao"

Judges 5:12

Taarifa ya jumla:

wimbo wa Debora na Baraka kwa kutumia ushairi unaendelea.

Amka, amka

Wazungumzaji wanaweza kuwa 1) wana wa Israeli au 2) Debora anajiambia mwenyewe au 3) mshairi aliyeandika wimbo.

Debora

Hili ni jina la mwanamke.

Baraka ... Abinoamu

Hya ni majina ya wanaume.

kwangu pamoja na mashujaa

"kwangu" inamaanisha Debora.

Judges 5:14

kutoka Efraimu, ambao mizizi yao iko katika Amaleki

Wana wa Efraimu waliokuwa wakiishi walikuwa uzao wa Amaleki.

walikufuata wewe

"wewe" inamaanisha watu wa Efraimu.

Mariki

Hili ni eneo ambalo uzao wa Mariki waliishi. Mariki alikuwa mwana wa Manase na mjukuu wa Yusufu.

kutoka Zebuloni wale wanaobeba fimbo ya afisa.

Viongozi wa kivita walitambulika kwa fimbo kama ishara ya mamlaka. "Kiongozi wa kivita wa Zebuloni"

Judges 5:15

Na wakuu wangu katika Isakari walikuwa pamoja na Debora

"wangu" ina maanisha Debora. Sentensi hii inaweza kuandikwa "Na wakuu wangu katika Isakari walikuwa pamoja nami"

Debora

Hili ni jina la mwanamke.

Isakari alikuwa na Baraka

"Isakari" ni kabila la Isakari.

Baraka

hili ni jina la mwanaume.

waliingia bondeni kwa kasi chini ya amri yake.

"kutii amri zake na kumfuata bondeni"

Kumfuata

"kumfuata nyuma kwa kasi"

kulikuwa na utafutaji mkubwa wa moyo.

"moyo" inawakilisha fikra. Watu kujadili wao kwa wao lakini wakashindwa kuamua nini cha kufanya inafananishwa na kutafuta mioyo yao.

Judges 5:16

Kwa nini uliketi katikati ya moto, ukisikiliza wachungaji wakipiga filimbi yao kwa makundi yao?

Hili swali limeulizwa ili kuwapinga wana wa Rubeni kwa sababu hawakuamua kwenda vitani. Pia inaweza kutafsiriwa "Mngetusaidia kupigana badala ya kukaa nyumbani na kusikiliza wachungaji wakipiga filimbi kwa makundi yao"

Moto

Tafsiri zingine za Biblia zinatafsiri "mazizi ya kondoo"

kulikuwa na utafutaji mkubwa wa moyo.

"moyo" inawakilisha fikra. Watu kujadili wao kwa wao lakini wakashindwa kuamua nini cha kufanya inafananishwa na kutafuta mioyo yao.

Judges 5:17

Gileadi alikaa

"Gileadi" inawakilisha watu wa Gileadi ambao walitakiwa kwenda vitani kupigana.

upande wa pili wa Yordani

Huuni upande wa mashariki wa Yordani.

na Dani, kwa nini alizunguka juu ya meli?

Swali hili liliulizwa ili kuelezea hasira kwa sababu watu wa Dani hawakupigana kwa ajili ya Israeli. "Na watu wa kabila la Dani hawakutusaidia vitani, badala yake walikuwa wakizunguka juu ya meli."

Dani, kwa nini

"Dani" inawakilisha watu wa Dani waliopaswa kwenda vitani kupigana.

kuzunguka juu ya meli

Kabila la Dani waliishi karibu na bahari ya Mediteraniani. Walifanya biashara kupitia bahari pamoja na uvuvi.

Asheri alibakia pwani na akaishi karibu na bandari zake

"Watu wa kabila la Asheri hawakutusaidia. walibaki pwani karibu na bandari zao."

Asheri alibaki

"Asheri" inawakilisha watu waliopaswa kwenda kwenda vitani kupigana.

Bandari

Pwani ya bahari yenye maji yenye kina kirefu ambapo meli huwekwa.

Naftali, pia

"Naftali lilikuwa kabila ambalo lilitoa maosha yake hata hatua ya kufa"

Judges 5:19

Wafalme walikuja, wakapigana ... wafalme wa Kanaani wakapigana

Mfalme wa kundi la watu hutumika kuelezea jeshi ambalo analiamuru.

Wakapigana ... wakapiagana

"Wakapigana nasi"

Taanaki ... Megido

Haya ni majina ya mahali

hakuna fedha kama nyara

"fedha" inawakilisha mali kwa ujumla.

nyara

Kitu kinachochukuliwa kwa nguvu, hasa katika vita au na wezi.

Nyota zilipigana kutoka mbinguni, kutoka katika njia zao za mbinguni zilipigana na Sisera

Bwana anawasaidia Waisraeli kumshinda Sisera na jeshi lake kama vile nyota zenyewe zinavyopigana na Sisera na jeshi lake. Mara nyingi Bwana hutumia vitu vya kawaida kama mvua ya radi kuipiga Sisera.

Dhidi ya Sisera

"Sisera" inawakilisha jeshi lake lote.

Sisera

Hili ni jina la mwanaume.

Judges 5:21

Mto Kishoni uliwaondoa

Kwa sababu ya mvua kubwa mto ulijaa haraka na ukasababisha magari yakwame kwenye tope na askari wengi kukwama.

Kishoni

Hili ni jina la mto.

Endelea mbele nafsi yangu, jipe nguvu

"nafsi" inamaanisha mtu. "yangu" ina maanisha Debora.

Kisha sauti za hofu za farasi-kupiga mbio, kupigana kwa watu wake wenye nguvu.

Hii inaelezea sauti ya farasi wengi wakikimbia toka vitani.

kupiga mbio

kukimbia haraka

Judges 5:23

Ilaani Merozi

"Merozi" inawakilisha watu waliokuwa wakiishi huko.

Merozi

Hili ni jina la mji.

Wenyeji

Watu waishio mahali fulani

Judges 5:24

Yaeli

Hili ni jina la mwanamke.

Heberi

Hili ni jina la mwanaume.

Mkeni

Moja ya mtu wa Keeni.

akamletea siagi

"siagi" ni maziwa mazito. Haya yalikuwa maziwa mazuri na kinywaji pendwa kwa watu wa Yaeli.

sahani inayofaa kwa wakuu

Hii inamaanisha kuwa sahani ile ilikuwa ya thamani sana kwa sababu wakuu walitumia vitu vya thamani.

Judges 5:26

Aliweka mkono wake kwenye kigingi cha hema

"Yaeli alitoa kigingi cha hema kwa mkono wake wa kushoto"

kigingi cha hema

Kipande cha mbao au chuma, kama sindano kubwa ambayo inachomekwa chini na kushikilia kona ya hema.

na mkono wake wa kuia katika nyundo ya mfanyakazi

"akachukua nyundo kwa mkono wake wa kulia"

Nyundo

Kifaa kizito kinachotumika kugongea kigingi cha hema chini.

Sisera

Hili ni jina la mwanaume

Akalala

Bila nguvu

aliuawa kwa ukatili

"alimuua" au "alikufa"

Judges 5:28

kamba

Huu ni mwonekano wa dirisha lililotengenezwa kwa mbao.

Kwa nini gari lake limechelewa kuja? Kwa nini viboko vya farasi vinavyovuta magari yake vimechelewa

Maswali haya yote yanamaana moja. "Kwa nini imemchukua Sisera mda mrefu kurudi nyumbani?"

gari lake limechukua ... nini viboko vya farasi vinavyovuta magari yake

Hivi vyote vinamuwakilisha Sisera. "Kumchukua Sisera ... kwa nini yeye"

Judges 5:29

Binti mfalme mwenye hekima

Huyu ni binti wa mfalme lakini pia anaweza kuwa mshauri wa kike wa familia ya kifalme.

akajibu jibu lile

"akajiambia mwenyewe kitu kile kile"

Je, hawakupata na kugawanya nyara?

"Watakuwa na nyara nyingi sana ndio maana wanachukua mda mrefu kugawana"

Tumbo, matumbo mawili kwa kila mtu ... kwa wale waliopora?

Wanawake wanatumia swali kusisitiza kuwa wanaamini hili ndilo lilitokea.

Tumbo, matumbo mawili kwa kila mtu

"tumbo" linawakilisha mwanamke. "Kila askari atapata mwanamke mmoja au wawili"

Nguo za rangi

"ngio zenye rangi"

Iliyofumwa

"imeshonwa vizuri"

misumari ya wale waliopora

"misumari" inawakilisha askari wa Sisera.

Judges 5:31

Waache wale wanaompenda

"Waache wale wanaompenda Bwana"

kama jua wakati linapoongezeka katika uwezo wake

Watu wa Israeli walitamani kuwa kama jua linapowaka kwa sababu hakuna jeshi lolote lenye nguvu ya kulizuia jua.

Nchi ilikuwa na amani

"nchi" inawakilisha watu wa Israeli.

Kwa miaka arobaini

"kwa miaka 40"

Judges 6

Judges 6:1

yaliyo mabaya machoni pa Bwana

"machoni mwa Bwana" inawakilisha kitu ambacho Bwana anakifikiria au kuwaza juu ya jambo fulani

mikononi mwa Midiani

"Midiani" inawakilisha watu wa Midiani. Pia "mkono" unawakilisha kutawala. "utawala wa watu wa Midiani"

Uwezo wa Midiani uliwanyanyasa Israeli

"uwezo wa Midiani" inamaanisha watu wa Midiani. "Watu wa Midiani walikuwa na nguvu kuliko watu wa Israeli na waliwanyanyasa"

Mabwawa

Eneo lenye miamba linaloweza kuwa makazi.

Judges 6:3

Waliweza kutengeneza jeshi

"Jeshi lao liliweka kambi" au "jeshi lao lilitengeneza hema"

Judges 6:5

Kila wakati wao na mifugo yao na mahema walipokuja

Nchi ya Midiani ilikuwa kusini mwa nchi ya Israeli pembeni mwa bahari ya Shamu.

walikuja kama kundi la nzige

Wamidiani wanafananishwa na kundi la nzige kwa sababu walikuja na kundi kubwa la watu na wanayama wao walikula kilakitu kilichopandwa.

Haikuwezekana kuhesabu

Hii inaonesha kuwa namba ilikuwa kubwa sana.

Midiani iliwadhoofisha

"Midiani" inawakilisha watu wa Midiani.

Wakamwita Bwana

"wakamwomba Bwana msaada"

Judges 6:7

walipomwomba Bwana

"wakamwomba Bwana msaada"

Kwa sababu ya Midiani.

"Midiani" inawakilisha watu wa Midiani.

Nimekuleta kutoka Misri

"Nimekuongoza kutoka Misri"

Nyumba ya utumwa

Musa anaizungumzia Misri kama nyumba ambayo watu waliwahifadhi watumwa. "sehemu ambayo mlikuwa watumwa"

Judges 6:9

Kutoka kwenye mkono

"mkono" unawakilisha nguvu na mamlaka.

Kutii sauti yangu

"sauti yangu" inawakilisha kitu ambacho Bwana ameamuru.

Judges 6:11

Sasa

Hapa msimuliaji anaanza kueleza sehemu mpya ya simulizi.

Malaika wa Bwana

Bwana anamtokea Gidioni kwa mfano wa malaika.

Ofra

Hili ni jina la mji.

Abiyezeri

Hili ni kundi la watu waliojiita baada ya babu yao Abiyezeri.

akitenganisha ngano katika sakafu

Hii ni hatua ya kupura nafaka. Gidioni alipura nafaka katika sakafu ili kutenganisha ngano na makapi.

Akamtokea

"akamwendea"

Judges 6:13

bwana wangu

Gidioni anatumia neno "bwana" kama njia ya unyenyekevu ya kumsalimia mgeni. Hakugundua kuwa anazungumza na Bwana kwa namna ya malaika.

Je, yako wapi matendo yake yote mazuri ambayo baba zetu walituambia, waliposema, 'Je! si Bwana aliyetukomboa kutoka Misri?'

Gidioni anatumia swali ili kuipinga sentensi ya mgeni kuwa Bwana yuko pamoja naye. Sentensi hii yaweza kuwa moja kwa moja kama "Hatujaona matendo makuu kama tuliyoambiwa na baba zetu kwamba Bwana aliwatoa Misri"

kututia mikononi mwa Midiani.

"kututia" inamaanisha Bwana aliruhusu Waisraeli washindwe.

kututia mikononi

"mkono" inawakilisha nguvu na utawala.

mwa Midiani

"Midiani" inawakilisha watu wa Midiani.

Judges 6:14

Bwana akamtazama.

"Bwana akamtazama Gidioni"

kutoka mkononi

"mkono inawakilisha nguvu au utawala.

Mwa Midiani

"Midiani inawakilisha watu wa Midiani"

Je, sikukutuma?

Bwana anatumia hili swali ili kumuhakikishia Gidioni kuwa amametuma. "kumtuma" inamaanisha kuwa Bwana amemchagua Gidioni kwa kazi maalumu.

Tafadhali, Bwana

Gidioni sasa anamuita Bwana. Inaonesha kuwa inaonekana Gidioni anatambua au anahisi kwamba anazungumza na Bwana.

Nawezaje kuwaokoa Israeli?

Gidioni aliuliza swali ili kusisitiza kuwa anafikiri hawezi kuwaokoa Waisraeli.

Tazama

"tafadhali elewa" au "sikiliza"

Katika Manase

"katika kabila la manase"

Katika nyumba ya baba yangu

"nyumba" inawakilisha familia. "katika familia ya baba yangu"

Judges 6:16

Nitakuwa pamoja nawe.

Hii inamaanisha kuwa Bwana atamsaidia na kumbariki Gidioni.

kama mtu mmoja

Hii yaweza kuwa na maana ya "itakuwa rahisi kama vile unapigana na mtu mmoja tuu.

kuiweka mbele yako

"kukuwekea mbele yako"

Judges 6:19

efa ya unga

Kama kuna ulazima wa kutumia njia za kisasa za kuonesha vipimo, hii ni moja wapo ya kufanya hivyo. "lita 22 za unga"

Mchuzi

Maji yaliyochanganywa na mboga kama vile nyama na kupikwa pamoja.

kumletea

"kumletea malaika wa Bwana"

Malaika wa Mungu.

Hii ni sawa na malaika wa Bwana. "Mungu aliye kama mfano wa Malaika"

Judges 6:21

Malaika wa Bwana.

Bwana akamtokea Gidioni kwa mfano wa Malaika.

Akaondoka

"akapotea"

Judges 6:22

Malaika wa Bwana

Bwana akamtokea Gidioni kwa mfano wa Malaika.

Ewe Bwana MUNGU!

"ewe" hii inaonesha kuwa Gidioni alikuwa na hofu.

nimemwona malaika wa Bwana uso kwa uso

Hii inaelezea namna ambavyo watuu wawili wapo karibu. "nimemwona kabisa malaika wa Bwana"

Bwana akamwambia

Bwana alizungumza na Gidioni toka mbinguni.

Hadi leo

Hii inamaanisha wakati ambao kitabu kitabu cha Waamuzi kimeandikwa.

Ofra

Hili ni jina la mji.

jamaa ya Abiezeri

Hili ni kundi la watu wa Abiezeri.

Judges 6:25

Ng'ombe wa pili

Hii inaonesha idadi kwamba kulikuwa na ng'ombe mwingine.

Karibu nayo

"karibu na madhabahu ya Baali"

juu ya mahali pa kukimbilia

Mji wa Ofra ulikuwa juu ya mlima. Waisraeli walikumbilia huko toka kwa Wamidiani ili wapate makazi.

kuijenga kwa njia sahihi

"weka matofali sehemu sahihi" au "ijenge vizuri"

Judges 6:27

Kufanya kama Bwana alivyomwambia

Hapa anatekeleza agizo la Bwana aliloambiwa katika 6:25

Judges 6:28

Alipoamka

"alipoinuka toka kitandani"

madhabahu ya Baali imebomolewa, na Ashera iliyokuwa karibu nayo imekatwa, na ng'ombe wa pili ametolewa sadaka kwenye madhabahu iliyojengwa

Hii inaweza kutafsiriwa kuwa "waligundua kuwa kuna mtu ameibomoa madhabahu ya Baali, akaikatakata Ashera iliyokuwa pembeni na akajenga madhabahu na kutoa kafara ng'ombe wa pili juu yake"

Judges 6:30

ili auawe

"tumuuwe kama adhabu"

Judges 6:31

Je, ninyi mtamsihi Baali?

Yoashi anatumia swali kusisitiza kuwa mwanadamu hatakiwi kuiokoa miungu.

Mtamsihi

"mtamtetea" au "mtatoa sababu"

Je mtamuokoa?

Yoashi anatumia swali kusisitiza kuwa mwanadamu hatakiwi kuiokoa miungu.

Yerubaali

Hili ni jina lingine la Gidioni likiwa na maana ya "Baali ajitetee mwenyewe"

Kwa sababu alisema.

"Kwa sababu Yoashi alisema"

Judges 6:33

Sasa

Hapa msimuliaji anaanza kueleza sehemu mpya ya simulizi.

Walikusanyika pamoja.

"walikusanyika pamoja kama jeshi"

Judges 6:34

Akaja juu ya Gideoni.

"kumtawala Gideoni"

Jamaa ya Abiezeri.

Hili ni kundi la watu wa Abiezeri.

ili wamfuate

"ili wamfuate katika vita"

na wao pia, waliitwa nje kumfuata

"waliitwa nje wamfuate"

Asheri, Zabuloni, na Naftali

Yote haya yanawakilisha watu wa kila kabila. "kabila la Asheri, Zebuloni na Naftali"

Judges 6:36

ngozi ya samazi

Nguo itokanayo na ngozi ya kondoo.

umande

maji yanayotoka kwenye mimea wakati wa usiku.

basi nitajua kwamba utanitumia

Maana halisi ya sentensi hii yaweza kuwa "Hii itakuwa ishara toka kwako, kisha nitajua kwamba utanituma"

Judges 6:38

Gideoni aliamka

Gideoni alitoka kitandani

akatoa

kukamua kitu au kusogeza ili kuondoa maji.

Judges 7

Judges 7:1

Yerubaali

Hili ni jina lingine la Gideoni.

Wakaweka kambi

"wakatengeneza kambi yao"

Chemchemi ya Harodi ... kilima cha More

Haya ni majina ya mahali.

Kambi ya Midiani ilikuwa kaskazini mwao

"Midiani" inawakilisha jeshi la Wamidiani. "Jeshi la Wamidiani liliweka kambi kaskazini mwa jeshi la Israeli"

Judges 7:2

kwa mimi kukupa ushindi juu ya Wamidiani

"kwa mimi kukuruhusu wewe uwashinde wa Midiani"

Nguvu zetu zimetuokoa

"nguvu" inawakilisha watu wenyewe. "Tumejiokoa wenyewe bila msaada wa Mungu"

Sasa

Hii haimaanishi "wakati huu" bali inatengeneza usikivu wa jambo muhimu linalofuata.

tangaza masikioni mwa watu

Neno "masikio" hapa linamaanisha mtu mwenyewe. "watangazie watu"

Yeyote anayeogopa, anayetetemeka

Maneno haya yote yana maana sawa.

Kutetemeka

neno hili linaelezea namna ambavyo hofu inaweza kusababisha mtu akatetemeka.

Muache arudi

"muache arejee nyumbani kwake"

Mlima Gileadi

Hili ni jina la mliama uliopo katika mji wa Gileadi.

Elfu ishirini na mbili

"22,000"

Elfu kumi wakabaki

"watu 10,000 wakabaki"

Elfu kumi

"10,000"

Judges 7:4

nitafanya idadi yao iwe ndogo kwa ajili yako

"idadi" inawakilisha jeshi. Sentensi hii yaweza kuwa "nitakuonesha ni akina nani wa kuwarudisha nyumbani ili jeshi liwe na watu kidogo"

Judges 7:5

Gideoni akawapeleka

"kuwapeleka" inaweza kutafsiriwa kama "kuwachukua" au "kuwaongoza"

kulamba

"kunywa maji kwa kuyalamba kutumia ulimi"

Watu mia tatu

"watu 300"

Judges 7:7

Watu mia tatu

"watu 300"

nitakuokoa na kukupa ushindi

Hapa alikuwa anamwambia Gideoni ila akimaanisha Gideoni na Waisraeli.

Kwa hiyo wale waliochaguliwa

"kwa hiyo wale waliochaguliwa na Bwana"

walichukua vifaa vyao na tarumbeta zao.

"zao" inawakilisha askari wa Israeli walioondoka kwenye jeshi.

Sasa

Hili ni nenp linalotumiwa na msimuliaji kuanza sehemu mpya ya simulizi.

Judges 7:9

Kavamie kambi, kwa maana nitakupa ushindi juu yake

"kambi" inamaana ya jeshi zima la Wamidiani.

Anaogopa kushuka

"anaogopa kwenda chini kuvamia"

Pura

Hili ni jina la mwanaume

ujasiri wako utaimarishwa

"Na unayoyasikia yatakupa ujasiri"

Sehemu ya walinzi

Sehemu ambayo askari husimama kutizama jeshi la adui.

Judges 7:12

wengi kama wingu la nzige

Hapa "wingu" inamaanisha kundi. Mwandishi analizungumzia jeshi kama kundi la nzige ili kusisitiza kuwa idadi ya askari ilikuwa kubwa.

Ngamia zao walikuwa zaidi ... kuliko idadi ya mchanga katika bahari.

Mwandishi anasisitiza kuonesha idadi kubwa ya ngamia waliokuwepo.

Ngamia zao walikuwa zaidi ya mawingu

"Ngamia zao zilikuwa nyingi na walishindwa kuzihesabu"

Judges 7:13

Hii si kitu kingine isipokuwa upanga wa Gideoni

"upanga wa Gideoni" inamaanisha jeshi la Gideoni linavamia. "mkate wa shayiri katika ndoto yako ni jeshi la Gideoni.

Mungu amempa ushindi juu ya Midiani

Hili tukio la baadae linazungumzwa kama vile ni tukio lililopita. Inasisitiza kuwa lazima itatokea.

Judges 7:15

Watu mia tatu

"watu 300"

Judges 7:17

Kwa Bwana na Gideoni

"Tunapigana kwa ajili ya Bwana na Gideoni"

Judges 7:19

Watu mia moja

"watu 100"

hapo mwanzoni mwa saa ya kati.

Mwanzoni mwa saa ya kati yaweza kuwa saa 10 kamili usiku.

Judges 7:20

Upanga wa Bwana na wa Gideon

"upanga" inamaanisha mapigano. "Tunapigana kwa ajili ya Bwana na Gideoni"

Judges 7:22

tarumbeta mia tatu

"tarumbeta 300"

Bwana akaweka upanga wa kila mtu wa Midiani dhidi ya wenzake

"Upanga" ina maanisha kuwa kushambulia kwao ni kwa kutumia upanga. "Bwana akasababisha kila Mmidiani kupigana na askari mwenzake"

Bethshita ... Serera ... Abel ... Mehola ...Tabathi

Haya ni majina ya miji.

Watu wa Israeli kutoka Naftali, Asheri, na Manase wote waliitwa nje

Hii yaweza kuwa "Gideoni waliwaita nje Waisraeli toka kwenye kabila la Naftali, Asheri na Manase.

Judges 7:24

Bethbara

Hili ni jina la mji.

walikusanyika pamoja na kumiliki maji, mpaka Bethbara na Mto Yordani

"na kumiliki eneo la mto Yordani mpaka Bethbara"

Orebu ... Zeebu

Haya ni majina ya wanaume.

mwamba wa Orebu ... katika shinikizo la divai la Zeebu

Haya ni maeneo ambayo yalipewa majina baada ya Waisraeli kumuuwa Orebu na Beebu.

Judges 8

Judges 8:1

Ni nini hiki umetutenda?

Watu wa kabila la Efraimu wanamkemea Gideoni kwa kutumia swali kwa kuwa hakuwaweka katika jeshi lake.

Dhidi ya Midiani.

"Midiani" inawakilisha jeshi la Midiani.

Wakamwambia kwa nguvu

"wakamwambia kwa hasira" au "wakamkemea kwa nguvu"

Judges 8:2

Taarifa ya jumla

Gideoni anawajibu watu wa Efraimu.

Nimefanya nini sasa kulinganisha na mlichofanya ninyi?

Gideoni anatumia swali kuonesha heshima kwa watu wa Efraimu. "Nimefanya mambo madogo gasa ukilinganisha na mliyofanya"

Je! Mavuno ya zabibu za Efraimu si bora zaidi kuliko mavuno ya zabibu ya Abiezeri?

"Mavuno ya Zabibu zenu watu wa Efraimu ni bora kuliko yetu sisi watu wa Abiezeri"

Je! Mavuno ya zabibu za Efraimu si bora zaidi kuliko mavuno ya zabibu ya Abiezeri?

Gideoni na jeshi lake kuwashinda Wamidiani kunafananishwa na mavuno ya zabibu. Watu wa Efraimi kumuua Orebu na Zeebu kunafananishwa na mavuno ya zabibu katika kipindi cha mavuno. "Jambo ambalo ninyi watu wa Efraimu mmefanya mwishoni mwa vita ni muhimu kuliko jambo ambalo sisi uzao wa Abiezeri tumefanya mwanzoni"

Abiezeri

Hili ni jina la mababu wa Gideoni. Gideoni alilitumia kuelezea uzao wa Abiezeri na nchi yao.

Orebu na Zeebu

Haya ni majina ya wanaume.

Mimi nimefanya nini ukilinganisha na ninyi?

Gideoni anatumia swali kuonesha heshima kwa watu wa Efraimu. "Nimefanya mambo madogo gasa ukilinganisha na mliyofanya"

Ikashuka chini

"ikapungua"

Judges 8:4

Watu mia tatu

"watu 300"

bado waliendelea kufuatilia

"Kufuatilia" ni neno ambalo linaweza kutumika kama "waliendelea kuwafukuza adui zao"

Zeba na Salmuna

Haya ni majina ya wanaume.

Judges 8:6

Je, mikono ya Zeba na Salmuna sasa ipo mikononi mwako?

Viongozi wanatumia swali kusisitiza kuwa Waisraeli bado hawajawakamata Zeba na Salmuna.

mikono ya Zeba na Salmuna

Hapa "mikono inamaanisha mwili mzima.

sasa ipo mikononi mwako

"mkono" inawakilisha nguvu na mamlaka.

Kwa nini tulipe jeshi lako mikate?

Viongozi wanatumia swali hili kusisitiza kuwa hawana sababu yoyote ya kuwapa mkate Waisraeli.

nitairarua ngozi yenu kwa miiba ya jangwani na michongoma.

Nitatengeneza mjeledi kwa kutumia miiba na michongoma ya jangwani na kuitumia kukupiga"

Miiba na michongoma

Vipande vyenye ncha kali vinavyokuwepo kwenye miti ambavyo vinaweza kuchoma watu au wanyama.

Judges 8:8

Akatoka huko

Hapa anazungumziwa Gideoni pamoja na askari waliomfuata. "Gideoni na watu 300 wakatoka huko"

Penieli

Hili ni jina la mahali.

akawaambia watu maneno hayo hayo

"akaomba chakula hapo kwa namna ile ile" au " pia akawaomba chakula"

Nitakapokuja kwa amani

Hii ni namna ya heshima ya kuzungumza juu ya kumshinda adui. "Baada ya kumaliza kulishinda jeshi la Midiani"

nitauangusha mnara huu

"Mimi" inawakilisha Gideoni na watu wake. "Watu wangu na mimi tutauangusha mnara huu"

Judges 8:10

Sasa

Hapa msimuliaji anaanza kusimulia sehemu nyingine mpya ya simulizi.

Zeba na Salmuna

Haya ni majina ya wanaume.

Karkori

Hili ni jina la mji.

Watu elfu kumi na tano

"watu 15,000"

watu waliofundishwa kupigana na upanga

Hii ni njia nyingine ya kuwaelezea askari

Na upanga

"upanga" inawakilisha upanga au silaha nyingine ambazo askari huzitumia vitani.

walianguka

Hii ni lugha ya upole inayomaanisha watu waliokufa vitani.

Judges 8:11

Gideoni akapanda

"Gideoni" inawakilisha askari wake wote. "Gideoni na askari wake"

Akalishinda

"Gideoni na jeshi lake wakalishinda"

Noba na Yogbena

Haya ni majina ya miji.

Zeba na Salmuna

Haya ni majina ya wanaume.

Hofu

Uwoga uliopitiliza unaosababisha mtu akashindwa kufikiri vizuri.

Judges 8:13

kupitia Heresi

Hili ni jina la barabara inayopita katikati ya milima miwili.

Akamkimbilia kijana mmoja

"akakutana na kijana mmoja"

kutafuta ushauri kutoka kwake

"Alimuomba amtajie majina ya viongozi wote wa mji"

Watu sabini na saba

"watu 77"

Judges 8:15

Zeba na Salmuna

Haya ni majina ya wanaume.

Je! mmemshinda Zeba na Salmuna?

Gideoni anarejea swali kwa watu wa Sukothi ili kuwakejeli. "Bado hamjamshinda Zeba na Salmuna."

Gideoni akawachukua ... naye akawaadhibu ... akaangusha

Hapa "Gideoni" anawakilisha askari wake.

Miiba na michongoma.

Vipande vyenye ncha kali vinavyokuwepo kwenye miti ambavyo vinaweza kuchoma watu au wanyama.

Penueli

Hili ni jina la mji.

Judges 8:18

Zeba na Salmuna

Haya ni majina ya wanaume.

Tabori

Hili ni jina la mji.

Kama wewe ulivyo, ndivyo walivyokuwa

"walikuwa kama wewe ulivyo"

Kama Bwana aishivyo

Hiki ni kiapo cha dini kinachoonesha kuwa anachotaka kuzungumza ni ukweli.

Judges 8:20

Yetheri

Hili ni jina la mtoto wa Gideoni.

kama mtu alivyo, ndivyo zilivyo nguvu zake

"Hii ni kazi ya mwanaume"

Makoja

Hili ni umbo ambalo hutokea wakati ambao mwezi umefunikwa kwa kiwango kikubwa na kivuli.

Mapambo

"mapambo"

Judges 8:22

wewe, mtoto wako, na mjukuu wako

Hii inaelezea kuwa walitaka uzao wa Gideoni kutawala juu yao baada ya yeye kufa.

umetuokoa mikononi mwa Midiani

"mkono" inawakilisha nguvu za Wamidiani juu ya Israeli.

Wamidiani

"Midiani" inawakilisha watu wa Midiani.

Judges 8:24

Gideoni akawaambia

"Gideoni akawaambia wana wa Israeli"

Hereni

dhahabu inayovaliwa sikioni

Nyara

Hivi ni vitu vilivyochukuliwa kwa nguvu au vilivyochukuliwa kwa watu waliokufa vitani.

Wamidiani walikuwa na pete za dhahabu kwa sababu walikuwa Waishmaeli

Hapa msimuliaji anatuelezea historia ya Wamidiani.

Vazi

Nguo kubwa inayotengenezwa kwa kipande kikubwa cha kitambaa na huvaliwa mabegani kama koti.

Judges 8:26

shekeli 1,700 za dhahabu

Ukitumia njia za kisasa kuonesha ukubwa wake yaweza kuwa "kilogramu 18.7 za dhahabu" au "karibu kilogramu 20 za dhahabu"

mapambo ya makoja

"mapambo"

Vidani

Ni pambo linaloning'inia shingoni.

Iliyovaliwa na wafalme wa Midiani.

"Ambazo Wafalme wa Midiani walivaa"

Judges 8:27

Gideoni akafanya efodi kutoka katika pete

"Gideoni alitumia dhahabu toka kwenye pete na kutengeneza efodi"

Ofra

Hili ni jina la mji.

Israeli wote wakaiandama kwa ukahaba na kuabudu

Kuabudu miungu ya uongo inafananishwa na ukahaba. "Waisraeli walimtenda Bwana dhambi kwa kuabudu efodi"

Waisraeli wote

Hii ni namna ya kusisitiza kuonesha kuwa idadi kubwa ya Waisraei waliabudu miugu.

Ilikuwa mtego kwa Gideoni na kwa wale walio nyumbani kwake.

Kuiabudu efodi inaelezwa kuwa ilikuwa mtego kwao. "ilikuwa jaribu kwa Gideoni na familia yake" au "Gideoni na familia yake walitenda dhambi kwa kuiabudu"

kwa wale walio nyumbani kwake

"nyumbani kwake" inawakilisha familia ya Gideoni.

Kwa hiyo Midiani ilishindwa mbele ya watu wa Israeli

Hii inaweza kuanza kama "Kwa hiyo Bwana akawafanya Wamidiani kushindwa mbele ya watu wa Israeli" au "kwa hiyo Bwana akawasaidia Waisraeli kuwashinda Wamidiani"

hawakuinua vichwa vyao tena

"Hawakuwavamia Waisraeli tena"

Na nchi ikawa na amani

"nchi" inawakilisha wana wa Israeli. "Na Waisraeli walikaa kwa amani"

Miaka arobaini

"miaka 40"

Siku za Gideoni

"siku" inamanisha kipindi cha uhai wake.

Judges 8:29

Yerubaali

Hili ni jina lingine la Gideoni.

Wana sabini

"wana 70"

Judges 8:32

uzee mzuri

"Alipokuwa mzee"

Akazikwa

Inaweza kuandikwa hivi "wakamzika"

Ofra

Hili ni jina la mji.

jamaa ya Abiyezeri

Hili ni kundi la watu toka katika uzao wa Abiezeri.

Ikawa

Hii hutumika kuonesha mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi. Kama lugha yako ina njia nyingine ya kufanya hivi unaweza kuitumia.

wakageuka tena

Watu walimkataa Bwana na hii imefananishwa na kitendo cha kugeuka toka kwake. "waliacha kumuabudu Bwana"

kujifanyia ukahaba wenyewe kwa kuabudu Mabaali

Kuabudu miungu ya uongo inafananishwa na ukahaba.

Baali Berith

Hili ni jina la mungu wa uongo

Judges 8:34

kutoka kwa mikono ya adui

"mkono" unawakilisha nguvu na utawala. "toka kwenye nguvu za adui zao wote"

Kila upande

"waliowazunguka"

Nyumba ya Yerubaali.

"nyumba ya" inawakilisha familia ya mtu.

Yerubaali

Hili ni jina lingine la Gideoni

Judges 9

Judges 9:1

Yerubaali

Hili ni jina lingine la Gideoni.

Tafadhali sema haya, ili wakuu wote wa Shekemu wasikie, Ni kipi bora kwako Je, wana sabini wote wa Yerubali kutawala juu yenu, au kwamba moja tu atawale juu yenu?

"Tafadhali waulize watu wa Shekemu kama wapo tayari kutawaliwa na wasa sabini wa Yerubaali au wana mmoja tuu atawale juu yao"

Sabini

"70"

mimi ni mfupa na nyama yenu.

"mifupa yenu na nyama yenu" inaelezea kuwa na undugu na mtu fulani.

Judges 9:3

Ndugu za mama yake waliongea kwa niaba yake kwa viongozi

Hii ina maana ya kwamba ndugu za mama yake Abimeleki walizungumza na viongozi, wakapendekeza wamfanye Abimeleki kuwa mfalme.

wakakubali kumfuata Abimeleki

"wakakubali Abimeleki awe kiongozi wao"

Nyumba

"nyumba" inawakilisha hekalu.

vipande sabini vya fedha

Hii inamaanisha shekeli. Shekeli ina uzito wa gramu 11. "karibia kilo moja ya fedha"

Sabini

"70"

Baali Berith

Hili ni jina la mungu wa uongo.

wasio na sheria na wajinga

"wakorofi na wajinga"

Judges 9:5

Ofra

Hili ni jina la mji.

Jiwe moja

"jiwe 1"

Sabini

"70"

Yerubaali

Hili ni jina lingine la Gideoni.

Beth Milo

Hili ni jina la mahali.

Judges 9:7

Taarifa ya jumla:

Yotamu anaanza kuelezea fumbo ambalo miti inafananishwa na makundi mbalimbali ya watu.

Yotamu alipoambiwa juu ya jambo hilo

"Yotamu aliposikia kuwa Abimeleki amemuua ndugu yake"

Mlima Gerizimu

Huu ni mlima.

Siku moja miti ilikwenda kumtia mafuta mfalme juu yao. Wakauambia mzeituni, tawala juu yetu.

Miti inazungumziwa kwa kufananishwa na watu.

kumtia mafuta mfalme juu yao

Kutia mafuta ni ishara ya kuwakilisha kitendo cha kumteua mtu kuwa mfalme.

Tawala juu yetu

"kuwa mfalme wetu"

Judges 9:9

Taarifa ya jumla:

Yotamu anaendelea kuelezea fumbo ambapo miti inawakilisha makundi mbalimbali ya watu.

mti wa mizeituni ukawaambia

Mti unafananishwa na mtu anayeweza kusikia na kuongea.

Je! Nitaacha mafuta yangu ... juu ya miti mingine?

Mzeituni unauliza swali la kukataa kuwa na huruma. Swali hili linaweza kuelezewa kama sentensi "Sitaacha mafuta yangu ... juu ya miti mingine"

Kuvuka juu

Mti unatumia maneno haya ukimaanisha "kutawala juu"

Mtini

Mti unafananishwa na mtu anayeweza kusikia na kuongea.

Je, nitaacha utamu wangu ... Je, nitaacha utamu wangu

Mtini unauliza swali la kukataa kuwa na huruma. "sitaacha utamu wangu ... juu ya miti mingine"

utamu wangu na matunda yangu

"utamu" ni neno linaloonesha kuwa matunda ya mti ule yamekomaa.

Judges 9:12

Taarifa ya jumla:

Yotamu anaendelea kuelezea fumbo ambapo miti inawakilisha makundi mbalimbali ya watu.

Mti ukasema

Mti unafananishwa na mtu anayeweza kusikia na kuongea.

Mzabibu

Mzabibu unafananishwa na mtu anayeweza kusikia na kuongea.

Je, nitaacha divai yangu mpya ... juu ya miti mingine?

Mzabibu unauliza swali la kukataa kuwa na huruma. "Sitaacha divai yangu mpya ... juu ya miti mingine."

Mti wa miiba

Hii ni miida ambayo ina ncha kali sana inayoumiza. kichaka hiki kina miiba mingi katika matawi yake.

Judges 9:15

Taarifa ya jumla:

Yotamu anaendelea kuelezea fumbo ambapo miti inawakilisha makundi mbalimbali ya watu.

Miti ya miiba

Miiba inafananishwa na mtu anayeweza kusikia na kuongea.

kunipaka mafuta niwe mfalme juu yako

Kupaka mafuta ni ishara ya kumteua mtu kuwa mfalme.

upate usalama

"uwe salama"

Acha moto utoke kwenye miti ya miiba

Hapa miti ya miiba inajielezea yenyewe. "acha moto utoke kwangu"

Acha moto utoke kwenye miti ya miiba na uiteketeze mierezi ya Lebanoni.

Hii inamaanisha acha miiba iwake moto ili iiteketeze mierezi.

Sasa

Hii inaleta umakini na kuonesha umuhimu wa jambo linalofuata.

ikiwa umefanya vizuri juu ya Yerubaali na nyumba yake, na ikiwa umemuadhibu kama anavyostahili

Yotamu anaonesha kuwa kwa namna moja walichokifanya ni kitu kizuri japokuwa Yotamu haamini moja kwa moja kuwa wamefanya jambo zuri.

Yerubaali

Hili ni jina lingine la Gideoni.

Nyumba yake

"nyumba" inawakilisha familia ya Gideoni.

Judges 9:17

Taarifa ya jumla:

Yotamu anafanya maombi juu ya hali iliyopo mda ule na sehemu ile.

na kufikiri kwamba baba yangu alipigana kwa ajili yenu ... kutoka kwenye mkono wa Midiani

Yotamu anaelezea ni kwa jinsi gani haamini vitendo vyao vibaya walivyovifanya watu wa Shekemu kwa Gideoni na familia yake japokuwa Gideoni alipigana ili kuwaokoa watu wa Shekemu.

kutoka kwenye mkono wa Midiani

"mkono" unawakilisha nguvu na utawala.

umeamka juu ya

"umeipinga" au "umeasi juu ya"

Nyumba ya baba yangu

"nyumba" inawakilisha familia.

Sabini

"70"

Jiwe moja

"jiwe 1"

Mtumishi wake wa kike

"wake" inasimama badala ya Gideoni.

Judges 9:19

Ikiwa mlifanya kwa uaminifu na uelekevu pamoja na Jerubalai na nyumba yake

Yotamu anaonesha kuwa kwa namna moja walichokifanya ni kitu kizuri japokuwa Yotamu haamini moja kwa moja kuwa wamefanya jambo zuri.

Yerubaali

Hili ni jina lingine la Gideoni

Nyumba yake

"nyumba" inawakilisha familia.

Lakini ikiwa sio

Yotamu anaonesha upande mwingine kuwa wakichokifanya ni makosa na anatoa laana. Yotamu anaamini kuwa walichokifanya ni makosa.

moto utoke kwa Abimeleki, ukawaangamize watu wa Shekemu

Yotamu anatoa laana. anazungumza juu ya Abimeleki kuwaharibu watu wa Shekemu kwa kuwaangamiza kwa moto.

Basi moto utoke kwa watu wa Shekemu na Beth Milo, ili kumteketeza Abimeleki.

Yotamu anatoa laana. anazungumza juu ya Shekemu na Beth Milo kumteketeza Abimeleki kwa kumuangamiza kwa moto.

Beth Milo

Hili ni jina la mahali.

Beeri

Hili ni jina la mji

Judges 9:22

tatu

"3"

Mungu alituma roho mbaya kati ya Abimeleki na viongozi wa Shekemu

Hii inamaanisha kuwa Mungu aliifanyia kazi laana aliyoitoa Yotamu kwa kutuma roho mbaya isababishe tatizo kati ya Abimeleki na viongozi wa Shekemu.

Mungu alifanya hivyo ili uhalifu uliofanywa ... walimsaidia kuua ndugu zake.

"Mungu alifanya hivi ili kulipiza kisasi cha wana sabini ambao waliuawa na Abimeleki na watu wa Shekemu wakamsaidia"

Sabini

"70"

Yerubaali

Hili ni jina lingine la Gideoni.

Judges 9:25

wakawaweka wanaume wakimsubiri juu ya vilima ili wamwangamize

"akatuma watu wajifiche kwenye vilima na wasubiri kumuangamiza Abimeleki"

Hii iliripotiwa kwa Abimeleki

"kuna mtu alimwambia Abimeleki kuhusu watu wanaomsubiri ili wamwangamize"

Judges 9:26

Gaali ... Ebedi

Haya ni majina ya wanaume.

walimwamini

Hiki ni kitendo cha kumwamini mtu.

Wakaenda shambani

Hapa Gaali na ndugu zake na watu wa Shekemu ndio wanaozungumziwa.

wakazikanyaga

Walifanya hivi ili kupata maji ya matunda ya mizabibu kwa ajili ya kutengeneza mvinyo.

kukanyaga

"kuponda"

katika nyumba

"nyumba" inawakilisha hekalu.

Judges 9:28

Gaali ... Ebedi

Haya ni majina ya wanaume.

Abimeleki ni nani, na Shekemu ni nani, hata tumtumikie?

Gaali anatumia swali kusisitiza kuwa watu wa Shekemu hawawezi kumtumikia Abimeleki.

Abimeleki ni nani, na Shekemu ni nani,

Maswali haya yanamaana moja. Gaali anamuelezea Abimeleki kama Shekemu maana mama yake na Abimeleki alitoka Shekemu.

Je, si mwana wa Yerubaali? Na Zebuli si afisa wake?

Gaali anatumia swali kusisitiza kuwa watu wa Shekemu hawawezi kumtumikia Abimeleki.

Yerubaali

Hili ni jina lingine la Gideoni.

Zebuli

Hili ni jina la mwanaume.

Watumikieni watu wa Hamori, baba yake Shekemu

Gaali anamaanisha watu wa Shekemu wawatumikie watu wa uzao wa Hamori.

Kwa nini tunapaswa kumtumikia?

Gaali anatumia swali kusisitiza kuwa watu wa Shekemu hawawezi kumtumikia Abimeleki.

Laiti watu hawa wangekukuwa chini ya amri yangu

"natamani ningekuwa nawatawala watu wa Shekemu"

Judges 9:30

Zebuli

Hili ni jina la mwanaume.

aliposikia maneno ya Gaali, mwana wa Ebedi

"maneno" inawakilisha kile alichokisema.

Gaali ... Ebedi

Haya ni majina ya wanaume.

hasira yake ikawaka

Kitendo cha kuwa na hasira kinafananishwa na moto unaoanza kuwaka.

ili wapate kudanganya

Zebuli anamdanganya Gaali na watu wa Shekemu.

nao wanauchochea mji dhidi yako

"wanawashawishi watu wa mji waasi dhidi yako"

mji

"mji" inawakilisha watu wa mjini.

Judges 9:32

Taarifa ya jumla:

Mjumbe wa Zebuli anaendelea kuzungumza na Abimeleki.

Sasa

Neno hili linaonesha umuhimu wa jambo linalofuata.

uvamizi

"kujificha na kushambulia ghafla"

fanyeni chochote mnachoweza

Hii inamaanisha wanaweza kufanya jambo lolote ili kuwaangamiza wafuasi wa Gaali.

Judges 9:34

watu wote waliokuwa pamoja

"na watu wote wakamsindikiza Abimeleki"

wakaandaa uvamizi dhidi ya Shekemu

"Shekemu" inawakilisha watu wa Shekemu.

wakagawanyika vitengo vinne

"wakagawanyika katika makundi 4"

Gaali ... Ebedi

Haya ni majina ya wanaume.

Judges 9:36

Gaali

Hili ni jina la mwanaume.

Zebuli

Hili ni jina la mwanaume.

Wewe unaona vivuli juu ya vilima kama vile watu

Zebuli anajaribu kumchanganya Gaali na kusababisha asijiandae na vita. "Hao sio watu ni vivuli tuu juu ya vilima"

kitengo kimoja

"kundi 1"

Judges 9:38

Zebuli

Hili ni jina la mwanaume.

Je, maneno yako ya kiburi yako wapi sasa?

"maneno" yanawakilisha kile alichosema. "kiburi chako kiko wapi sasa."

wewe uliyesema, 'Abimeleki ni nani, ili tumtumikie?

Zebuli ananukuu swali la Gaali kwa Gaali mwenyewe. "wewe ndiye uliyesema kwamba tusimtumikie Abimeleki."

Je, hao sio watu ambao uliwadharau?

Swali hili linaweza kuwekwa katika senytensi kama "Hawa ndo watu ambao uliwadharau"

Aliwadharau

"aliwachukia" au "hakuwapenda"

Gaali

Hili ni jina la mwanaume

Na wengi wakaanguka na majeraha ya mauti

"na wengi wakafa kwa sababu ya majeraha"

Judges 9:41

Aruma

Hili ni jina la mji.

Zebuli

Hili ni jina la mwanaume.

Gaali

Hili ni jina la mwanaume.

hii ikamfikia Abimeleki

"kuna mtu alimfikishia taarifa Abimeleki"

akawagawanywa katika vitengo vitatu

"Akawatenganisha kati ka vitengo 3"

wakaandaa uvamizi mashambani

"Walijificha mashambana na kuwavamia watu ghafla.

Akawakamata

Huyu ni Abimeleki anayewakilisha askari wake.

Judges 9:44

vitengo

"Makundi ya askari"

vingine viwili

"vingine 2"

Abimeleki alipigana ... Akabomoa

"Abimeleki" anawakilisha askari wake. "Abimeleki na askari wake walipigana... wakabomoa"

Dhidi ya mji

"mji" inawakilisha watu. "dhidi ya watu wa Shekemu"

Akabomoa

Akaharibu

kueneza chumvi juu yake

Kitendo cha kumwaga chunvi juu ya nchi ni kitendo cha kuzuia kitu chochote kisistawi hapo"

Judges 9:46

nyumba

Hii inawakilisha hekalu.

El Berithi

Neno "El" inamaana ya mungu. Hili ni jina la mungu wa uongo.

Abimeleki aliambiwa

"kuna mtu alimwambia Abimeleki"

Judges 9:48

Mlima Salmoni

Hili ni jina la mlima.

Wakayafungia

Kuyashikiza na kuyafunga pamoja.

Elfu moja

"1,000"

Judges 9:50

Thebezi

Hili ni jina la mji

akapiga kambi dhidi ya Thebezi

"akapiga kambi nje ya mji wa Thebezi"

Judges 9:52

kupigana nao

"kuwavamia"

jiwe la juu

Mawe makubwa mawili yaliyokuwa yanatumika kusagia nafaka. Jiwe la juu ni lile lililokuwa juu ambalo lilizungushwa ili kusaga nafaka.

mbeba silaha

Huyu ni mtu aliyekuwa anabeba silaha za Abimeleki.

akamchoma

Hii inamaanisha kuwa kijana alichomeka upanga kwenye mwili wa Abimeleki.

Judges 9:55

Sabini

"70"

akafanya uovu wote wa watu wa Shekemu ugeuke juu ya vichwa vyao wenyewe

"uovu wao ukawarudia juu ya vichwa vyao" "kuwaadhibu watu wa Shekemu kwa uovu waliofanya"

juu yao ilikuja laana ya Yothamu mwana wa Yerubaali

"laana ya Yothamu mwana wa Yerubaali ikawapata"

Yerubaali

Hili ni jina lingine la Gideoni.

Judges 10

Judges 10:1

Tola ... Pua ... Dodo

Haya ni majina ya wanaume.

Shamiri

Hili ni jina la mahali.

akaondoka ili kuwaokoa Israeli

"akaenda kuwaokoa Israeli" au "akawa kiongozi na kuwaokoa Israeli"

kuwaokoa Israeli

"Israeli" inawakilisha watu wa Israeli.

Akawa mwamuzi wa Israeli

"kuamua" inamaanisha kuwaongoza watu wa Israeli.

Miaka ishirini na tatu

"Miaka 23"

Akazikwa

"wakamzika"

Judges 10:3

Alifuatiwa na Yairi Mgileadi

"Yairi Mgileadi alikuwa kiongozi baada ya Tola"

Yairi

Hili mi jina la mwanaume.

Mgileadi

Yairi alitoka katika kabila la Gileadi.

Akawa mwamuzi wa Israeli.

"kuamua" inamaanisha kuwaongoza watu wa Israeli.

Israeli

"Israeli" inawakilisha watu wa Israeli.

Miaka ishirini

"miaka 20"

Thelathini

"30"

Hawoth Yairi

Hili ni jina la mji lililotokana na jina la mtu.

hata leo

Hii inamaanisha wakati ambao kitabu cha waamuzi kinaandikwa.

Akazikwa

"wakamzika"

Kamoni

Hili ni jina la mahali.

Judges 10:6

waliendelea kutenda maovu mbele za Bwana

"waliendelea kufanya mambo ambayo Bwana alisema ni uovu"

mbele za Bwana

"mbele za Bwana" inawakilisha kitu ambacho Bwana anakifikiria au kuwaza juu ya jambo fulani.

Maashtoreti

Huu ni wingi wa Ashtoreti aliyekuwa anaabudiwa kama mungu wa uongo kwa namna mbalimbali.

Wakamsahau Bwana na hawakamsujudia tena

"waliacha kabisa kumwabudu Bwana"

Wakamsahau Bwana

Kumtii na kumwabudu Bwana inazungumzwa kama kitendo cha watu kumwacha Bwana na kwenda mahali pengine.

Hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli

Kitendo cha Bwana kuwa na hasira kinafananishwa na moto uwakao.

akawauza mikononi mwa Wafilisti na katika mikono ya wana wa Amoni

Bwana akaruhusu Wafilisti na Waamoni wawashinde Waisraeli.

mkononi mwa

"mkono" unawakilisha nguvu na utawala.

Judges 10:8

Kuwaangamiza na kuwadhulumu

Haya maneno mawili yana maana moja ya kusisitiza ni kwa namna gani wana wa Israeli walikuwa wanateseka.

Miaka kumi na nane

"miaka 18"

waliokuwa ng'ambo ya Yordani

Hii inamaanisha waliokuwa mashariki mwa mto Yordani.

iliyoko Gileadi

"huu mji pia uliitwa Gileadi"

Yuda ... Benyamini

"Yuda" na "Benyamini" inasimama badala ya watu waliotoka katika makabila haya. "watu wa kabila la Yuda ... watu wa kabila la Benyamini"

Nyumba ya Efraimu

"nyumba" inasimama badala ya kabila la Efraimu.

Israeli akasumbuliwa sana

"israeli" inasimama badala ya watu wa Israeli. "watu wa Israeli wakateseka sana"

Judges 10:10

wana wa Israeli wakamwita Bwana

Hii ina maana kuwa wana wa Israeli waliomba msaada kwa Bwana.

kwa sababu tumemwacha Mungu wetu

Watu waliacha kumtii na kumuabudu Bwana, walimuacha na kwenda kuabudu miungu mingine.

tumemwacha Mungu wetu

"kukuacha wewe, Mungu wetu"

Je, sikuwatoa ninyi ... Wasidoni?

Bwana aliwakemea wana wa Israeli kwa kitendo chao cha kuabudu miungu mingine.

Waamoni

Hawa ni watu wa familia ya Amoni.

kutoka katika nguvu zao

"Nguvu" inawakilisha Waamaleki na Wamaoni.

Judges 10:13

mliniacha tena

Watu waliacha kumtii na kumuabudu Bwana, walimuacha na kwenda kuabudu miungu mingine.

Kwa hiyo, sitawaokoa tena.

"Sitaendelea kuwaokoa tena na tena"

Judges 10:15

Wakaiacha miungu ya kigeni

Watu wakaacha kuabudu miungu ya uongo.

miungu ya kigeni waliyokuwa nayo

"miungu ya kigeni ambayo walimiliki sanamu zake"

Naye akawa na subira juu ya taabu ya Israeli.

"Naye hakutaka watu wa Israeli wateseke tena"

Judges 10:17

Ni nani atakayeanza kupigana na Waamoni?

"Nani ataongoza jeshi letu ili kupigana na Waamoni?"

Judges 11

Judges 11:1

Mgileadi

Huyu ni mtu anayetoka katika mji wa Gileadi.

Wana wa mkewe walipokua

"Wana wa mke wa Gileadi walipokuwa wakubwa"

nchi ya Tobu

Hili ni jina la mji.

wakaja na kwenda pamoja naye.

"wakamfuata" au "walienda kila sehemu pamoja"

Judges 11:4

Siku kadhaa baadae

"Siku zilizofuata"

walipopigana na Israeli

Waliwashambulia Waisraeli na kupigana vita pamoja nao.

ili tupigane na

"ili tupigane dhidi ya"

Judges 11:7

Nyumba ya baba yangu.

"nyumba" inawakilisha watu waishio nyumbani.

Ndiyo sababu tunakugeukia sasa

"tunakuja kwako sasa kwa sababu tupo kwenye shida"

pigana na watu wa Amoni

"pigana dhidi ya watu wa Amoni"

Judges 11:9

msimamizi na mkuu

Maneno haya yana maana moja na yanasisitiza ni kwa namna gani Yeftha alikuwa wa muhimu.

Alipokuwa mbele ya Bwana huko Mizpa, Yeftha akarudia ahadi zote alizozifanya.

"mbele ya Bwana" inamaanisha kuwa alirudia ahadi zake kama kiapo mbele za Bwana.

ahadi zote alizozifanya

Hizi ni ahadi alizozitoa kwa viongozi wa Gileadi kwa kuwa kiongozi wao.

Judges 11:12

Ni nini mgogoro huu kati yetu?

"Kwa nini kuna mgogoro kati yetu?" Yeftha anamuuliza mfalme kwa nini wana hasira na Israeli.

Kwa nini umekuja kwa nguvu kuchukua ardhi yetu?

"Kwa nini askari wako wamekuja kuchukua ardhi yetu"

umekuja kwa nguvu kuchukua

"kuja kuchukua kwa nguvu"

Arnoni ... Yaboki

Haya ni majina ya mito miwili.

mpaka Yordani

"Upande mwingine wa mto Yordani"

Kwa amani

"amani"

Judges 11:14

Akasema

Mjumbe ndiye anayezungumza na mfalme. "Yeftha alimwambia mjumbe aseme"

walitoka Misri

Waisraeli walipotoka Misri walikuwa njiani kuelekea katika nchi ya ahadi.

Judges 11:17

Taarifa ya jumla:

Mjumbe wa Yeftha anaendelea kuzungumza.

Israeli walipotuma wajumbe

Wajumbe hawa walitumwa na viongozi wa Israeli.

Kupita

"kipitia" au "kukatisha"

Walikataa

"kukataa" au "kutosikiliza ombi lao"

Wakawatuma wajumbe kwa mfalme wa Moabu

"pia walituma wajumbe kwa mfalme wa Moabu juu ya ombi hilo hilo"

lakini akakataa

Mfalme wa Moabu alikataa ombi la Waisraeli kupita katika Moabu.

Arnoni

Hili ni jina la mto.

Judges 11:19

Taarifa ya jumla:

Mjumbe wa Yeftha anaendelea kuzungumza.

Israeli wakatuma wajumbe kwa Sihoni

Wajumbe walitumwa na viongozi wa Israeli.

Sihoni

Hili ni jina la mtu.

Heshboni ... Yahasa

Haya ni majina ya miji.

Lakini Sihoni hakumwamini Israeli apite katika eneo lake

Sihoni hakumuamini Israeli apite katika nchi yake kwa amani.

Akapigana huko

Sihoni anawakilisha jeshi lake. "wakapigana huko" au "jeshi lake likapigana huko"

Judges 11:21

Taarifa ya jumla:

Mjumbe wa Yeftha anaendelea kuzungumza.

Sihoni

Hili ni jina la mwanaume.

akamtia Sihoni na watu wake wote mkononi mwa Israeli

"mkono" inamaanisha nguvu ya kushinda vitani.

Arnoni ... Yaboki

Haya ni majina ya mito.

Judges 11:23

Taarifa ya jumla:

Mjumbe wa Yeftha anaendelea kuzungumza.

na sasa mnataka kuimiliki nchi yao?

"kwa hiyo hamtakiwi kuchukua umiliki wa nchi yao."

Je, huwezi kuchukua nchi ambayo Kemoshi, mungu wako, anakupa?

Yeftha anamkemea mfalme wa Waamoni kwa kutumia swali. "mlipaswa kuchukua ardhi ambayo mungu wenu Kemoshi amewapa."

kuchukua

"kumiliki" au "kutawala"

Kemoshi

Hili ni jina la mungu wa uongo.

Sasa wewe ni bora zaidi kuliko Balaki, mwana wa Sipori, mfalme wa Moabu?

Yeftha anamkemea mfalme wa Waamoni kwa kutumia swali. "wewe sio bora kama Balaki mwana wa Sipori mfalme wa Moabu."

Balaki ... Zipori

Haya ni majina ya wanaume.

Je, alidai kuwa na hoja na Israeli?

Yeftha anamkemea mfalme wa Waamoni kwa kutumia swali.

Je, yeye amewahi kupigana vita dhidi yao?

Yeftha anamkemea mfalme wa Waamoni kwa kutumia swali. "Hakupigana vita dhidi yao."

Judges 11:26

Taarifa ya jumla:

Mjumbe wa Yeftha anaendelea kuzungumza.

Miaka mia tatu

"miaka 300"

Heshboni

Hili ni jina la mji.

Aroeri

Hili ni jina la mji.

Arnoni

Hili ni jina la mji.

kwa nini hamkuwachukua tena wakati huo?

"Mngewachukua tena wakati huo" au "sasa mmechelewa; mngewachukua wakati huo."

ijawafanyia vibaya, lakini mnanifanyia vibaya kwa kunishambulia

Yeftha anazungumza na Sihoni. "Waisraeli hawajakufanyia mabaya, lakini watu wako wanatutendea mabaya kwa kutushambulia.

kuwatenda mabaya ... kunitendea mabaya

Kumtendea mtu mabaya inamaana kumfanyia mtu jambo baya.

Judges 11:29

Roho wa Bwana akamjia Yeftha

"Roho wa Bwana akamtawala Yeftha"

akapita Gileadi na Manase ... kutoka Mispa ya Gileadi

Yeftha alipita maeneo haya akiorodhesha watu kwa ajili ya jeshi lake kwenda vitani na watu wa Amoni.

Nami nitatoa hiyo sadaka

Kutoa kitu kwa ajili ya sadaka. "Nitakitoa kwako"

Judges 11:32

Basi Yeftha akapita kwa ... Bwana akampa ushindi ... Akawashinda

"Basi Yeftha na jeshi lake wakapita kwa ... Bwana akawapa ushindi ... wakavamia"

Aroeri

Hili ni jina la mji.

Minithi ... Abeli Keramimu

Haya ni majina ya miji.

Miji ishirini

"Miji 20"

Judges 11:34

Ngoma

Hiki ni kifaa cha muziki kinachopigwa kwa kutumia vipande vya chuma.

alirarua nguo zake

Hiki ni kitendo cha kuonesha kuomboleza au huzuni kubwa.

Umenivunja kwa huzuni ... umekuwa mtu anayenisababishia maumivu yangu

"Yeftha anazungumza kitu kile kile kusistiza ni kwa kiasi gani aamehuzunika"

Umenivunja kwa huzuni

Yeftha anaizungumzia huzuni yake kama vile kitu kilichovunjwa. "Umenisababishia huzuni kubwa"

umekuwa mtu anayenisababishia maumivu yangu

Yeftha anazungumza juu ya shida aliyonayo akiifananisha na maumivu.

siwezi kurudisha ahadi yangu.

Yeftha hawezi kuacha kufanya alichoahidi kukifanya.

Judges 11:36

amekulipia kisasi juu ya adui zako, wana wa Amoni

"amekulipa kisasi juu ya adui zako, wana wa Amoni kwa kuwashinda wao"

Hebu ahadi hii ihifadhiwe kwa ajili yangu

"Itunze ahadi hii kwa ajili yangu" au "itunze ahadi hii kuhusu mimi"

kuomboleza juu ya ubikira wangu

"kuomboleza kwa sababu mimi ni bikira" au "kuomboleza kwa sababu sitaolewa"

Judges 11:38

Mgileadi

Yairi alitoka katika kabila la Gileadi.

Judges 12

Judges 12:1

Watu wa Efraimu walitoka pamoja

"Watu wa Efraimu waliitwa pamoja" au "Watu wa Efraimu waliwakusanya askari wao"

Zafoni

Hili ni jina la mji.

wakapitia ... umetangulia

"kusafiri kupitia" au "kusafiri"

Tutachoma nyumba yako.

Hii inamaanisha tutachoma moto nyumba yako na watu walioko ndani.

Nilipokuita,

Hii imetumika kama wingi ikimaanisha watu wa Efraimu.

hukuniokoa

Hapa Yeftha anawaelezea watu wa Gileadi kama yeye mwenyewe. "hamkutuokoa sisi"

Judges 12:3

hamkuniokoa

Yeftha anawazungumzia watu wa Gileadi pamoja na yeye mwenyewe.

nikaweka uhai wangu na nguvu yangu mwenyewe

Hii inamaanisha kuyatoa muhanga maisha yako na kutegemea nguvu zako mwenyewe.

Bwana alinipa ushindi

Yeftha anaonesha kuwa Bwana aliwapa ushindi watu wa Gileadi juu ya Waanoni.

akapigana na Efraimu

Yeftha na watu wote wa Gileadi walipigana na Efraimu.

Kwa nini mmekuja kupigana nami leo?

Yeftha inamaanisha watu wa Gileadi. "Kwa nini mmekuja kupigana nasi"

Ninyi Wagileadi ni wakimbizi

"ninyi Wagileadi hapa sio kwenu. Mmekuja hapa kuishi tuu"

kupita ili kupigana na wana wa Amoni

Hii inamaanisha walipigana na Waamoni walipokuwa wakipita Amoni.

Wagileadi

"watu kutoka Gileadi"

katika Efraimu-katika Efraimu na Manase

"katika mji wa Efraimu na manase" au "katika nchi ya Efraimu na Manase"

Judges 12:5

kwa Efraimu

"katika nchi ya Efraimu"

Wagileadi waliteketeza

"Wagileadi walitawala"

Vivuko

Sehemu ambazo unaweza kupita kuvuka mto kwa miguu.

Mwefraimu

"Mtu toka kabila la Efraimu"

Shiboleth ... 'Sibboleth

Maneno haya hayana maana yoyote.

kutamka

"sema"

Elfu arobaini na mbili

"42,000"

Waefraimu elfu arobaini na mbili waliuawa

"Waliwaua Waefraimu elfu arobaini na mbili"

Judges 12:7

Yeftha Mgileadi akafa na akazikwa

"Yeftha Mgileadi akafa na wakamzika"

Judges 12:8

Ibzani

Hili ni jina la mtu toka Betlehemu.

Aliwapeleka binti thelathini katika ndoa

Hii inamaanisha aliwaruhusu binti zake kuolewa.

naye akaleta binti thelathini kutoka nje kwa ajili ya wanawe

"aliandaa mabinti thelathini toka nje ya jamaa yake kwa ajili ya kuolewa na watoto wake wa kiume"

Judges 12:10

Alizikwa Bethlehemu.

"wakamzika Bethlehemu"

Eloni

Hili ni jina la mwanaume.

Mzabuloni

Mtu kutoka kabila la Zabuloni.

Aiyaloni

Hili ni jina la mahali.

akazikwa huko Aiyaloni

"wakamzika huko Aiyaloni"

Judges 12:13

Abdoni ... Hileli

Haya ni majina ya wanaume.

Mpirathoni ... Pirathoni

Pirathoni ni jina la mahali, na mtu anayetokea huko anaitwa Mpirathoni.

Walipanda punda sabini

Watu hawa walimiliki punda sabini ambao waliwapanda.

wana arobaini ... wajukuu thelathini ... punda sabini

"wana 40 ... wajukuu 30 ... punda 70"

Judges 13

Judges 13:1

yaliyo mabaya machoni pa Bwana

"machoni pa Bwana" inawakilisha kitu ambacho Bwana anakifikiria au kuwaza juu ya jambo fulani.

akawatia mikononi mwa Wafilisti

"mkono" inamaanisha nguvu ya kushinda vitani. "aliruhusu Wafilisti wawashinde"

Miaka arobaini

"miaka 40"

Sora

Hili lilikuwa jina la mji katika Israeli. Ilikuwa katika mji wa Yuda karibu na mpaka wa Dani.

Wadani

Watu wa kabila la Dani.

Manoa

Hili ni jina la mwanaume.

Judges 13:3

kuzaa mtoto mwanaume.

"kuzaa mtoto wa kiume" au "kuwa na mtoto wa kiume"

chochote kilicho najisi

Kitu ambacho Bwana amesema hakifai kuliwa kinaonekana kuwa ni najisi.

Tazama

"sikiliza"

Hakuna wembe itakayotumiwa juu ya kichwa chake

"kichwa" inamaanisha nywele. "Hakuna mtu atakayekata nywele zake"

Wembe

Ni kisu kikali kitumikacho kukata nywele karibu na ngozi.

Mnaziri wa Mungu

"alitolewa kwa Mungu kama Mnaziri"

kutoka tumboni

"kabla hajazaliwa"

mkono wa Wafilisti

"mkono" inamaanisha utawala. "kuwa chini ya utawala wa Wafilisti"

Judges 13:6

Mtu wa Mungu

Hii inamaanisha kuwa mtu huyu alitumwa na Mungu.

kuonekana kwake kulikuwa kama malaika wa Mungu, wa kutisha sana.

"Nilimwogopa kwa sababu alionekama kama malaika wa Mungu"

Tazama

"sikia"

Utazaa mtoto mwanaume

"kuzaa mtoto wa kiume" au "kuwa na mtoto wa kiume"

chakula chochote ambacho sheria inasema kuwa si safi

Kitu ambacho Bwana amesema hakifai kuliwa kinaonekana kuwa ni najisi.

Mnaziri wa Mungu.

"alitolewa kwa Mungu kama Mnaziri"

tangu alipokuwa tumboni mwako mpaka siku ya kufa kwake

Hii inasisitiza kuwa itakuwa hivi kwa kipindi chote cha maisha yake.

Judges 13:8

Manoa

Hili ni jina la mwanaume.

akamwendea mwanamke

"akamwendea mke wa Manoa"

Judges 13:10

Tazama

"Sikia" au "tega sikio na ninayotaka kukwambia"

Mtu

Hii inamaanisha malaika wa Mungu.

Judges 13:12

Maneno yako

Haya ni maneno ambayo yule mtu aliyasema. "maneno uliyosema"

kitu chochote kinachotokana na mizabibu

Hapa malaika anamaanisha chakula chochote kitokanacho na mizabibu.

chochote ambacho sheria inasema kuwa si safi

Kitu ambacho Bwana amesema hakifai kuliwa kinaonekana kuwa ni najisi

Judges 13:15

kuandaa mbuzi kwa ajili yako

"kupika mbuzi kwa ajili yako ili upate kula"

Judges 13:17

maneno yako yatakapotimia

"maneno yako" haya ni maneno ambayo malaika aliyasema.

Mbona unauliza jina langu?

Malaika anamuuliza swali kwa kumkemea. swali hili laweza kuwa "Hupaswi kuniuliza jina langu"

Ni ajabu

"Ni ajabu kwako kuelewa"

Judges 13:19

sadaka ya nafaka

Sheria hii inataka sadaka ya nafaka itolewe wakati sadaka ya kuteketezwa inatolewa.

juu ya mwamba

"juu ya madhabahu"

Alifanya jambo

"Malaika alifanya jambo"

malaika wa Bwana akapanda katika moto wa madhabahu

"malaika wa Bwana akarudi mbinguni kupitia miale ya moto juu ya madhabahu"

wakainamisha vichwa vyao chini

Hii ni ishara ya utii na heshima lakini pia inaonesha walikuwa na hofu ya Bwana.

Judges 13:21

kwamba yule ndiye malaika wa Bwana

"yule" inamuelezea yule mtu ambaye Manoa na mke wake walimuona.

Hakika tutakufa, kwa sababu tumemwona Mungu

"Mungu atatufanya tufe kwa sababu tumemuona yeye"

Judges 13:23

Asingetuonesha mambo haya yote, wala wakati huu asingeweza kuturuhusu tusikie mambo hayo.

Mke wa manoa alizungumza jambo lile lile.

Judges 13:24

Mwanamke

"Mke wa Manoa"

kuzaa mtoto mwanaume

"kuzaa mtoto wa kiume" au "kuwa na mtoto wa kiume"

alikua

"akawa kijana" au "akapevuka"

Roho wa Bwana akaanza kumchochea

"Roho wa Bwana akaanza kumchochea Samsoni"

Mahane Dani ... Eshtaoli

Mahane Dani ni jina la kambi ya muda ambayo kabila la Wadani waliishi hapo wakiwa wanatafuta makazi ya kudumu.

Sora

Hili ni jina la mji.

Judges 14

Judges 14:1

Samsoni akashuka kwenda Timna

Neno "kushuka" linatumika kwa sababu Timna ipo juu ya ilipokuwa nyumba ya baba yake na Samsoni. Timna ni jina la mji uliopo kwenye bonde la Soreki.

mmojawapo wa binti za Wafilisti.

"binti" ni njia moja wapo ya kuelezea kuwa mwanamke huyu alikuwa hajaolewa.

Sasa mkanichukulie awe mke wangu.

Samsoni aliwaomba wazazi wake wazungumze na wazazi wa yule mwanamke kuhusu ndoa.

Judges 14:3

Je, hakuna mwanamke kati ya binti za ndugu zako, au kati ya watu wetu wote?

Waliuliza swali kwa kutoa maoni kuwa wanaweza kumtaftia Samsoni mke kati ya jamaa zao.

binti za ndugu zako

"binti" ni njia moja wapo ya kuelezea kuwa mwanamke huyu alikuwa hajaolewa.

Je! Utachukua mke kutoka kwa Wafilisti wasiotahiriwa?

Swali hili linaulizwa ili kumkemea Samsoni. "Hutakiwi kuoa mwanamke wa Kifilisti kwa sababu Wafilisti hawamwabudu Bwana"

Nichukulie kwa ajili yangu

Samsoni aliwaomba wazazi wake wazungumze na wazazi wa yule mwanamke kuhusu ndoa.

Ananipendeza mimi

Samsoni alifikiri kuwa binti yule ni mzuri. "Ananipendeza kwa namna alivyo mzuri"

suala hili

Hili ni ombi la Samsoni kuoa wanamke wa Kifilisti.

kwa maana alitaka kutengeneza mgogoro na Wafilisti

Kwa maana Bwana alitaka kutengeneza mgogoro na Wafilisti.

Judges 14:5

Samsoni akashuka Timna

Neno "kushuka" linatumika kwa sababu Timna ipo juu ya ilipokuwa nyumba ya baba yake na Samsoni. Timna ni jina la mji uliopo kwenye bonde la Soreki.

Na, tazama, kuna simba mdogo wa alikuja

"Tazama" ni neno lililotumika ili kumfanya msomaji awe makini kwa tukio linalofuata katika simulizi.

alikuwa akiunguruma

"alikuwa akimtisha." Hii ni sauti ya simba ambayo huitoa akiwa anataka kuvamia kitu.

Roho wa Bwana ghafla akaja juu yake

Roho wa Bwana akamchochea Samsoni. Akamfanya kuwa na nguvu sana.

Kumrarua ... vipande

Akamrarua vipande viwili.

hakuwa na kitu mkononi mwake

Hakuwa na kitu mkononi mwake ikimaanisha kuwa hakuwa na silaha yoyote.

Judges 14:7

alimpendeza Samsoni

Samsoni anafikiri kuwa binti yule ni mzuri. "Ananipendeza kwa namna alivyo mzuri"

Akageuka

Hii inamaanisha aliiacha njia na kufanya jambo fulani.

Mzoga

"Kiumbe kilichokufa"

Na, tazama, kulikuwa na kundi la nyuki

"Tazama" ni neno lililotumika ili kumfanya msomaji awe makini kwa tukio linalofuata katika simulizi. "

Kundi

"kundi kubwa la wadudu"

Akaweka

"akakusanya"

Judges 14:10

Baba yake Samsoni akaenda chini alipokuwa mwanamke

Neno "kushuka" linatumika kwa sababu Timna ipo juu ya ilipokuwa nyumba ya baba yake na Samsoni. Hapa inaonesha kuwa alikuwa Timna pamoja na Samsoni.

desturi ya vijana

"desturi ya vijana waliokaribia kuoa"

rafiki zao thelathin

"rafiki zao 30"

Judges 14:12

Kitendawili

Huu ni mchezo ambao wachezaji wanatakiwa wagundue jibu kutokana na swali gumu.

anaweza kuipata

"Anaweza kuipata maana yake"

nguo za kitani thelathini na seti ya nguo thelathini

"nguo za kitani 30 na seti ya nguo 30"

Lakini ikiwa hamuwezi kuniambia

Anawaambia maneno haya wageni waliokuwa kwenye sherehe.

Kitani

Aina ya nguo.

Judges 14:14

Taarifa ya jumla:

Samsoni anawaambia kitendawili.

Kati ya mtu aliyekula kilikuwepo kitu cha kula

"kitu cha kula kilikuwepo ndani ya mtu aliyekula"

"aliyekula"

Inaweza kuelezewa kama "kitu kinachokula"

nje ya nguvu kilikuwa kitu tamu

"Kitu ambacho ni kitamu kimetoka kwenye kitu chenye nguvu"

yenye nguvu

"kitu chenye nguvu"

Wageni wake

"watu waliokuwepo kwenye shherehe"

Hawakupata jibu

"Hawakugundua jibu"

Judges 14:15

siku ya nne

"siku ya 4"

mdanganye

Kumdanganya mtu afanye jambo ambalo hataki kufanya.

Nyumba ya baba yako

Hii yaweza kuwa na maana ya 1) inamaanisha nyumba kabisa. 2)"nyumba" inamaanisha watu wanaoishi ndani yake.

Tutachoma moto

"kuchoma moto" inamaanisha kukiteketeza kutu kwa moto. Kama mtu akichomwa moto inamaana mtu huyo ameteketea kwa moto mpaka kufa.

Je, umetualika hapa ili kutufanya maskini?

Wanamuuliza swali hili kwa kumshataki kuwa amewaalika ili awafanye maskini. "umetuleta hapa ili kutufanya maskini"

kutufanya maskini

Watakuwa masikini kama watamnunulia nguo mpya ikiwa watashindwa kutegua kitendawili.

Judges 14:16

Yote unayoyafanya ni kunichukia! Hunipendi

"Hunipendi mimi kabisa"

Kitendawili

Huu ni mchezo ambao wachezaji wanatakiwa wagundue jibu kutokana na swali gumu.

Angalia hapa

"angalia" inamanisha "sikiliza" "nisikilize mimi" au "kuwa makini kwa ninachotaka kukwambia"

kama sijawaambia baba yangu au mama yangu, nikuambie wewe?

Samsoni anamkemea mke wake baada ya mkewe kumlazimisha amwambie jibu.

kwa siku saba ambazo sikukuu yao iliendelea

Yaweza kuwa na maana ya 1)"katika siku saba za sikukuu yao" au 2) "katika siku saba zilizobaki za sikukuu yao"

Siku ya saba

"siku ya 7"

Alimlazimisha sana

"Aliendelea kumlazimisha ili amwambie"

Judges 14:18

Siku ya saba

"siku ya 7"

Watu wa mji

Hawa ni ndugu wa mke wa Samsoni.

Ni nini kilicho bora zaidi kuliko asali? Ni kitu gani chenye nguvu kuliko simba?

Hili ndilo jibu la kitendawili. "asali ni tamu na simba ni mkali" au "asali ni tamu na imetoka kwa simba"

Ikiwa hamkulima na ng'ombe wangu

Samsoni anafananisha kumtumia mke wake kupata jibu kama kutumia ng'ombe wa mtu kulima shamba lake. "Kama msingemtumia mke wangu"

Kulima

Hiki ni kitendo cha kutumia mnyama kuvuta jembe kuandaa ardi kwa ajili ya kuweka mbegu.

Judges 14:19

akaja kwa Samsoni kwa nguvu

"akaja" hii inamaanisha kuwa roho wa Bwana alimchochea Samsoni. "akamfanya Samsoni kuwa na nguvu sana"

Akawauwa watu thelathini

"Akawauwa watu 30"

watu hao

"watu walioishi hapo"

Nyara

Vitu vinavyochukuliwa kwa nguvu, hasa baada ya mapigano vitani.

Seti ya nguo

"Seti ya nguo alizochukua"

alikasirika

"kukasirika sana"

akaenda nyumbani kwa baba yake

Samsoni alikuwa Timna ambapo kulikuwa juu kuliko sehemu ambayo nyumba ya baba yake ilikuwepo.

Na mke wake akachukuliwa na rafiki yake

"baba wa mke wake alimkabidhi kwa rafiki yake wa karibu"

Rafiki wa karibu

"rafiki wa karibu"

Judges 15

Judges 15:1

Akajiambia mwenyewe

"Akafikiri mwenyewe"

Nitaenda kwenye chumba cha mke wangu

"Nitaenda kwenye chumba cha mke wangu ili tulale pamoja"

hakumruhusu aingie

"jakumpa ruhusa aingie chumbani kwake"

hivyo nikampatia rafiki yako

"Hivyo nikampa aolewe na rafiki yako"

Je sio?

Anauliza swali hili kuonesha kuwa Samsoni anapaswa kukubali. "Natumaini unakubali"

Mchukue badala yake

"Mchukue awe mke wako badala yake"

Judges 15:3

sitakuwa na hatia juu ya Wafilisti wakati nikiwaumiza

Samsoni anafikiri kuwa kwa sababu Wafilisti wamemkosea hivyo hatakuwa na hatia akiwavamia.

Mbweha mia tatu

"mbweha 300"

Mbweha

Mbweha ni wanayama wadogo kama mbwa wenye mikia mirefu wanaokula wanyama wadogo wadogo na ndege.

Kila jozi

Jozi ni vitu viwili. Mfano mbweha wawili au mikia miwili.

Mkia kwa mkia

"kwa mikia yao"

Taa

Ni fimbo ya mbao inayowaka na kutoa mwanga ambayo mara nyingi hutumika usiku.

Judges 15:5

Nafaka

Nafaka ambazo zinaendelea kukua katika shamba.

Nafaka

Nafaka zilizokusanywa kabla hazijavunwa.

Mashamba

Hii ni sehemu ambayo miti ya matunda inakua.

Mtimna

Ni mtu anayetoka Timna.

Mkwe wa Mtimna

"mkwe"

alimchukua mke wa Samsoni akampa rafiki yake

"akamchukua mke wa Samsoni na kuruhusu aolewe na rafiki yake"

Wakamchoma

Hii inaonesha kuwa mtu alichomwa moto mpaka kufa.

Judges 15:7

akawaambia

"akawaambia Wafilisti"

Ikiwa ndivyo mnavyofanya

"kwa sababu mnafanya hivi"

akawakata vipande vipande, paja na mguu

"Akakata miili yao vipande vipande"

akashuka chini

"akashuka chini" au "akaenda"

pango

Sehemu ya wazi iliyopo mlimani.

Mwamba

mwamba uliopo kwenye mlima.

Etamu

Hili ni jina la mwamba karibu na Yerusalemu.

Judges 15:9

Wafilisti wakaja ... huko Yuda

Wafilisti walienda Yuda ambapo ni juu toka kwenye nchi yao.

kujiandaa na vita

"kujipanga wenyewe kwa ajili ya vita"

Lehi

Hili ni jina la mji uliopo Yuda.

tumtendee kama alivyotutendea

"tumuuwe kama alivyowaua watu wetu"

Judges 15:11

Watu elfu tatu wa Yuda

"watu 3,000 wa Yuda"

mwamba la Eatamu

Hili ni jina la mwamba lililopo karibu na Yerusalemu.

Je, hujui kwamba Wafilisti hutawala juu yetu? Je! umetutendea nini?

"Unajua kwamba Wafilisti wanatutawala lakini unafanya kama vile hawatutawali. Unayoyafanya yanatusababishia madhara makubwa."

Kwa kadiri walivyonitendea mimi, vivyo hivyo nimewatendea wao.

"Wamemuua mke wangu hivyo nimewaua na wao"

Judges 15:12

mikononi mwa Wafilisti

"Mikono" inamaanisha nguvu. "utawala wa Wafilisti"

kukupeleka kwao

"kukupeleka kwa Wafilisti"

kutoka kwenye mwamba

Huu ni mwamba wa Eatamu ambao Samsoni alienda.

Judges 15:14

Alipofika

"Samsoni hakusafiri pekeyake, alikuwa akiongozwa na watu waliokuwa wamemfunga kwa kamba"

Lehi

Hili ni jina la mji uliopo Yuda.

akaja juu yake kwa nguvu

Roho wa Bwana alimchochea Samsoni. "akamfanya Samsoni kuwa na nguvu"

Kamba zilizokuwa juu ya mikono yake zikawa kama kitambaa cha kuteketezwa

"Alizikata kamba zilizokuwa mikononi mwake kwa urahisi kama kitambaa kilichokuwa kinateketezwa"

Kitambaa

Hiki kimetokana na mmea ambacho hutumika kutengenezea nyuzi na nguo.

Judges 15:15

mfupa mbichi

Hii inamaanisha kuwa punda alikufa siku za karibuni na mfupa wake haukuanza kuharibika.

watu elfu moja

"watu 1,000"

taya ya punda

"taya ya punda"

Chungu juu ya chungu

Maneno haya yanaelezea ni kwa namna gani Samsoni aliwaua watu wengi sana.

Judges 15:17

Ramath Lehi

Hili ni jina la mahali. Lenye maana ya kilima cha taya.

alikuwa na kiu sana

"alihitaji maji ya kunywa"

Lakini sasa nitakufa kwa kiu na kuanguka

Yaweza kuwa na maana ya 1)Samsoni alikuwa na kiu sana kiasi cha kufa. 2)Samsoni alitia chunvi kuonesha ni kwa kiasi gani alikuwa na kiu.

kufa kwa kiu

Hii inamaanisha kuwa kufa kwa sababu hujanywa maji ya kutosha hivyo hauna maji ya kutosha mwilini.

kuanguka mikononi mwa wale wasiootahiriwa?

"kuanguka mikononi" Hii inamaanisha kukamatwa. "Wasiotairiwa" hawa ni Wafilisti, hii inasisitiza kuonesha kuwa hawakumwabudu Bwana.

Judges 15:19

akapafungua mahali pa shimo

"akapafungua mahali pa shimo" Hii ni sehemu ya chini ambayo Bwana alisababisha maji ya chemchemi yatoke.

Lehi

Hili ni jina la mji uliopo Yuda.

nguvu zake zikarejea na akahuishwa

"akapata nguvu tena" au "nguvu zake zikarejea"

Enhakore

Hili ni jina la chemchemi.

ni huko Lehi hadi leo

"chemchemi ipo mpaka leo huko Lehi"

katika siku za Wafilisti

"Katika wakati wa Wafilisti kuwatawala Waisraeli"

miaka ishirini

"miaka 20"

Judges 16

Judges 16:1

akalala pamoja naye

"Akalala naye"

Watu wa Gaza wakaambiwa

"Kuna mtu aliwaambia watu wa Gaza"

Watu wa Gaza wakazunguka mahali hapo ... wakamngoja usiku wote katika lango la jiji

Hii inaonesha kuwa Wagaza walizunguka sehemu ambayo Samsoni alikuwepo na wengine wakasubiri katika lango la jiji ili asiondoke.

Walikaa kimya usiku wote

"Hawakupiga kelele zozote usiku kucha" au "hawakutaka kumkamata usiku"

Judges 16:3

Usiku wa manane

"katikati ya usiku"

Miimo miwili

Yawezekana ilitengenezwa kwa magogo ya miti na ilichimbiwa chini ya ardhi kwa ajili ya kusikilia malango ya jiji.

Komeo na vyote

Komeo ni kifaa kizito cha chuma kinachounganishwa na mlango.

mabega

Hii ni sehemu ya mwili wa binadamu ambapo mikono na shingo vimeunganishwa pamoja.

Hebroni

Hili ni jina la mji.

Judges 16:4

Bonde la Sereki

Hili ni jina la bonde lililokuwa karibu na nyumba ya Samsoni.

Danganya

ni kitendo cha kumpotosha mtu ili afanye jambo ambalo hataki kufanya.

ili uone

"ili uelewe" au "ili ujifunze"

mahali zilipo nguvu zake kuu

"kinachomsababisha awe na nguvu"

kwa namna gani tunaweza kumshinda

"kwa jinsi gani tunaweza kumshinda"

Judges 16:6

kukufunga, ili aweze kukudhibiti

"kukufunga ili kukudhibiti"

kamba safi

Kamba hutengenezwa kwa kutumia wanyama. kamba safi ni zile ambazo zimetoka kwa mnyama ambaye amechinjwa na hajakauka bado.

ambazo hazijakauka

"ambazo hazijawa kavu"

Judges 16:8

ambazo hazijakauka

"ambazo hazijawa kavu"

akamfunga Samsoni

"Delila akamfunga Samsoni na kamba safi"

Sasa

Mwandishi anatueleza simulizi kuhusu Wafilisti na Delila wanavyosubiri kumkamata Samsoni.

Wafilisti wako juu yako

"Wafilisti wako hapa ili kukukamata"

akazikata kamba kama uzi wakati unapogusa moto

Mwandishi anaelezea ni kwa jinsi gani ilikuwa rahisi kwa Samsoni kuzikata kamba kama vile zinavyokatika zikiwa katika moto.

Judges 16:10

Ndivyo ulivyonidanganya mimi ... kuniambia uongo

"Umenidanganya"

Unaweza kufungwa

"watu wanaweza kukushinda"

Wafilisti wako juu yako

"Wafilisti wako hapa ili kukukamata"

waliokuwa wakisubiri

"wakimsubiri ili kumshambulia"

kama kilikuwa kipande cha uzi.

Mwandishi anaelezea ni kwa jinsi gani ilikuwa rahisi kwa Samsoni kuzikata kamba akifananisha na kipande cha uzi.

Judges 16:13

umenidanganya na kuniambia uongo

"Umenidanganya"

unaweza kufungwa

"watu wanaweza kukushinda"

Kufuma

Kupishanisha vipande pamoja ili vishikane.

vifungo vya nywele zangu

Vipande vidogo vya nywele

Kitambaa

nguo iliyotengenezwa kwa kufuma.

Kitanda cha mfumi

Hii ni mashine inayochanganya nyuzi na kutengeneza nguo.

kisha ukafunga kwenye kitanda cha mfumi

"kisha ukafunga kitambaa kwenye kitanda cha mfumi"

kufunga

Kufunga kitu sehemu moja.

nitakuwa kama mtu mwingine yeyote

"Nitakuwa na udhaifu kama mtu mwingine"

Wafilisti wako juu yako

"Wafilisti wako hapa ili kukukamata"

akang'oa kitambaa na pini zilizokuwa zimefungwa

"alizitoa nywele zake, pamoja akang'oa na pini zilizokuwa zimefungwa na kitambaa kilichokua kwenye kitanda cha mfumi"

Judges 16:15

Wawezaje kusema, 'Unanipenda', wakati hushiriki siri zako na mimi

Delila anauliza hili swali akiwa na maana ya kuwa kama Samsoni anampenda kwa dhati alipaswa kumwambia siri zake.

alisisitiza kwa bidii ... akamkemea sana

Hapa mwandishi anaonesha ni kwa kiasi gani Delila alimsisitiza Samsoni ili amwambie anachotaka kukifahamu.

na maneno yake

Haya ni maneno aliyosema Samsoni kwa Delila.

alitamani kufa

Hapa mwandishi ametia chunvi kuonesha ni jinsi gani Samsoni alichoshwa na maneno ya Delila.

Judges 16:17

alimwambia kila kitu

Alimwambia kila kitu juu ya asili ya nguvu zake.

wembe

Hiki ni kifaa chenye makali kinachotumika kinyolea nywele.

Mnaziri wa Mungu.

"alitolewa kwa Mungu kama Mnaziri"

kutoka tumboni mwa mama yangu

"kabla sijazaliwa"

Ikiwa kichwa changu kitanyolewa

"kama mtu atanyoa kichwa changu"

Kunyoa

Ni kitendo cha kukata nywele.

nguvu zangu zitaniacha

"sitakuwa na nguvu tena"

Judges 16:18

Delila alipoona

"kuona" inamaana ya alipotambua.

ukweli juu ya kila kitu

"ukweli juu ya nguvu za Samsoni"

Njooni tena

Delila anawaambia viongozi waende anapoishi.

wakaleta fedha mkononi mwao

Hii inamaanisha kuwa walimleta fedha walizomuahidi kuwa watampa ikiwa atawasaidia kumkamata Samsoni.

Alimfanya alale

"Alimsababisha alale usingizi"

kwenye mapaja yake

"alilaza kichwa chake kwenye mapaja yake"

Paja

Paja ni eneo la mguu wa juu.

Vifungo saba vya nywele zake

Samsoni alikuwa na vifungo saba katika nywele zake.

kumshinda

"kumtawala"

nguvu zake zilikuwa zimemwacha.

"nguvu zake ziliondoka" au "hakuwa na nguvu tena"

Judges 16:20

Wafilisti wako juu yako, Samsoni

Wafilisti wamekuja kukukamata.

Aliamka

"kuamka"

Nitatoka nje

"nitatoroka"

wakamng'oa macho yake

Hiki ni kitendo cha kutoa macho yake.

Wakampeleka Gaza.

Gaza ni sehemu iliyokuwa chini toka kwenye nyumba waliyomkamata.

wakamfunga kwa shaba

"wakamfunga kwa kutumia shaba"

Pingu

Hivi ni vifungo vinavyofungwa mwisho wa minyororo ili kushikilia miguu na mikono ya mfungwa.

Akisaga ngano

"kusaga ngano kuzunguka duara"

Jiwe la kusagia

Hili ni jiwe kubwa lenye umbo la duara ambalo hutumika kusagia nafaka. Huwa linazunguswa na wanyama kama ng'ombe au farasi.

baada ya kunyolewa.

"Baada ya Wafilisti kuzinyoa"

Judges 16:23

Dagoni

Alikuwa mungu wa uongo wa Wafilisti.

amemshinda

"amemshinda"

kumtia katika ufahamu

Mwandishi anaonesha kuwa Samsoni alikuwa chini ya utawala wa Wafilisti.

mharibifu wa nchi yetu

"mtu aliyeharibu nchi yetu"

aliwaua wengi wetu

"mtu aliyeua watu wetu"

Judges 16:25

Mwite Samsoni ... Walimwita Samsoni

Kwa kuwa Samsoni alikuwa mfungwa hakuitwa moja kwa moja, bali watu walimuomba mtu aliyekuwa muhusika ili amlete Samsoni.

Kijana

Huyu hakuwa mtoto mdogo lakini alikuwa kijana.

Niruhusu nishike nguzo zilizoshikilia nyumba hii, ili nipate kuegemea

"Niruhusu nishike nguzo zilizoshikilia nyumba"

Judges 16:27

Sasa

Hapa mwandishi anaelezea taarifa fulani kwa kukatisha simulizi.

wanaume na wanawake elfu tatu

"wanaume na wanawake 3,000"

Wakiangalia

"wakitazama"

wakati Samsoni alipokuwa akiwafurahisha

"Wakati Samsoni akiwafurahisha." "kufurahisha" ni kitendo cha kusimama katikati ya watu na kuwafanya wafurahi na kucheka.

Judges 16:28

Akamwita Bwana

"Akamwomba Bwana"

Nipe nia

"nikumbuke mimi"

mara moja tu

"kwa mara nyingine"

kwa wakati mmoja

Hii inamaanisha Samsoni anataka kulipiza kisasi ;lakini ili ikamilike inahitaji kitendo kimoja cha ngubu ambacho ni kuziangusha nguzo.

ambazo zinashikilia nyumba

"ambazo zinaishikilia jengo"

Judges 16:30

Alisukuma kwa nguvu zake

"alitumia nguvu zake kusukuma nguzo"

Waliouawa

"watu waliokufa"

walikuwa zaidi

"idadi yao ilikuwa kubwa sana"

nyumba yote ya baba yake

"familia yote ya baba yake"

Kisha ndugu zake na nyumba yote ya baba yake wakashuka

"Walishuka" kwa sababu sehemu ambayo familia ya Samsoni walitoka ilikuwa juu ya Gaza.

Sora ... Eshtaoli

Haya ni majina ya mahali.

mahali pa kuzikwa Manoa, baba yake

"mahali alipozikwa Manoa baba yake"

Manoa

Hili ni jina la mwanaume.

Samsoni alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka ishirini

"Samsoni alikuwa mwamuzi wa Israeli kwa miaka ishirini kabla hajafa"

Miaka ishirini

"miaka 20"

Judges 17

Judges 17:1

Kulikuwa na mtu

Hii ni njia ya kumtambulisha mtu mwingine katika simulizi.

Mika

Hili ni jina la mwanaume.

ambazo zilichukuliwa kutoka kwako

"ambazo mtu aliziiba toka kwako"

Nimeziiba

"mimi ndiye niliyezichukua"

Judges 17:3

Nimeweka

Hii inamaanisha kuweka kitu kwa ajili ya kusudi maalumu.

takwimu za chuma

Chuma kilichoyeyushwa na kutengeneza umbo maalumu.

Nakurudishia wewe

"Nairudisha kwako"

Vipande mia mbili vya fedha

"vipande 200 vya fedha"

Vikawekwa ndani ya nyumba ya Mika

"Mika akaviweka ndani ya nyumba yake"

Judges 17:5

nyumba ya sanamu

Hii ni nyumba ambayo ni maalumu kwa ajili ya kuabudu sanamu. "alikuwa na nyumba ya kuabudia sanamu"

kila mtu alifanya yaliyo sawa machoni pake.

"kila mtu alifanya kile alichoona kilikuwa sawa"

Judges 17:7

Wa Bethlehemu

"toka Bethlehemu"

wa jamaa ya Yuda

Hii inamaana kuwa alikuwa akiishi kati ya familia ya Yuda, ambalo ni kabila la Yuda.

Alikaa huko ili kutimiza majukumu yake

"Alikaa na kufanya kazi huko"

kutafuta mahali pa kuishi

"kutafuta sehemu tofauti ya kuishi"

nipate kuishi

"ambapo nitaishi na kupata kazi"

Judges 17:10

baba na kuhani

Hapa "baba" imetumika kama mshauri. "mshauri na kuhani"

suti ya nguo

"suti ya nguo kila mwaka"

Basi Mlawi akaingia nyumbani mwake

"Hivyo Mlawi akakubaliana na alichoambiwa na akaingia kwenye nyumba yake"

huyo kijana kwa Mika akawa kama mmoja wa wanawe

Uhusiano kati ya Mika na Mlawi ukawa wa karibu sana kama uhusiano wa baba na mtoto wake.

Judges 17:12

Mika akamtenga Mlawi

"Kumtenga" maana yake ni kumtoa. "Mika akamtoa Mlawi"

katika nyumba ya Mika

"aliishi katika nyumba ya Mika"

Judges 18

Judges 18:1

Siku hizo ... miongoni mwa makabila ya Israeli

Haya ni maelezo juu ya Israeli na watu wa kabila la Dani.

Siku hizo

Hii inaonesha mwanzo wa tukio katika simulizi.

hawakupokea urithi wowote kutoka

"hawakupokea ardhi kama urithi"

kutoka kwa idadi yote ya kabila lao

"idadi yote" inamaanisha watu wa kabila lile.

wenye ujasiri

"wenye uzoefu wa kupigana"

ili kukagua ardhi kwa miguu

"miguu" inamaanisha kutembea.

Sora

Hili ni jina la mji.

Eshtaoi

Hili ni jina la mji.

Mika

Hili ni jina la mtu.

Judges 18:3

walitambua maneno ya Mlawi

Walimtambua yule mtu kwa namna alivyoongea.

Judges 18:7

Laishia

Hili ni jina la mji.

Hapakuwa na mtu aliyewashinda katika nchi hiyo

"Hapakuwa na adui yeyote aliyeishi kwenye nchi yao na kuwashinda"

hawakuwa na ushirikiano na mtu yeyote

"hawakuwa na mawasiliano na mtu yeyote wa nje" Hii inamaanisha kuwa walikuwa mbali sana na miji mingine.

Zora

Hili ni jina la mji.

Eshtaol

Hili ni jina la mji.

Judges 18:9

Je hamfanyi kitu?

Hili ni swali lenye maana ya kuwa mnapaswa kufanya jambo. "Mnapaswa kuchukua hatua sasa"

Msiwe wavivu kushambulia

"Shambulieni haraka"

nchi ni pana

"Nchi ni kubwa"

hapajapungukiwa kitu chochote duniani

"tutakuwa na kila kitu tunachokitaka"

hakujapungukiwa

"kuna kila kitu"

Judges 18:11

Watu mia sita

"watu 600"

Kiriath-yearimu

Hili ni jina la mji.

Mahane Dani

Hili ni jina la mji.

hata leo

Hii inamaanisha kuwa kitu kile kipo vile vile. "na mpaka leo ndio jina lake"

Judges 18:13

Laisha

Hili ni jina la mji.

Je, mnajua kwamba katika nyumba hizi kuna efodi ... sanamu za chuma? Amua utakachofanya.

Watu watano waliuliza hili swali kama njia ya kupendekeza na kuwahimiza wenzao ili waibe zile sanamu.

Judges 18:15

Wakarudi huko

"wakarudi"

wakamsalimu

"wakamsalimu Mlawi"

Wadani mia sita

"Wadani 600"

Judges 18:17

Watu mia sita

"Watu 600"

Judges 18:19

Je, ni bora kuwa wewe kuhani kwa ajili ya nyumba ya mtu mmoja ... jamaa katika Israeli?

"Ni vizuri kwako kuwa kuhani wakabila na jamaa wa Israeli kuliko kuwa kuhani wa mtu mmoja"

Moyo wa kuhani ulifurahi

"Kuhani alifurahi"

Judges 18:21

Wameweka watoto wadogo mbele yao wenyewe

Walisafiri kwa namna hii ili kuwalinda watoto.

umbali mzuri

Huu sio umbali mrefu lakini unatosha kupima namna mnavyoendelea.

watu waliokuwa ndani ya nyumba zilizo karibu na nyumba ya Mika waliitwa

"Mika aliwaita watu waliokuwa wakiishi katika nyumba zilizokuwa karibu na nyumba yake"

wakawafikia Wadani

"waliwakimbilia Wadani na wakawafikia"

wakageuka

"Wadani wakageuka"

Kwa nini mmewaita pamoja?

"Msingewaita watu wenu pamoja ili kutukimbiza"

mmewaita pamoja

"mmewaita watu hawa pamoja"

Judges 18:24

miungu niliyoifanya

Mika hakuitengeneza miungu lakini fundi aliitengeneza.

Je, nina nini tena?

"sijabakiwa na kitu" au "mmechukua kila kitu ambacho ni muhimu kwangu"

Unawezaje kuniuliza, 'Ni nini kinachokusumbua?

Mika anauliza hili swali akiwa na maana kuwa Wadani wanafahamu kitu kinachomsumbua.

Usiruhusu tusikie chochote unachosema

"Usirihusu tukagundua chochote ulichozungumza" au "usiseme chochote juu ya hili"

Kusikia ukisema chochote

"kukusikia ukisema chochote juu ya swala hili"

familia yako mtauawa

"na kuiuwa familia yako"

wakaenda zao

Hii ina maana ya kuwa wakaendelea na safari yao.

walikuwa na nguvu sana juu yake

Wadani walikuwa na nguvu sana juu ya Mika na watu wake.

Judges 18:27

kile alichokifanya Mika

Mika hakuitengeneza miungu lakini fundi aliitengeneza.

Laisha

Hili ni jina la mji.

kwa upanga

"upanga" unawakilisha upanga au silaha nyingine zinazotumiwa na askari vitani.

hawakuwa na uhusiano na mtu yeyote

Hii inamaanisha kuwa walikuwa wakiishi mbali na miji mingine hivyo walikuwa mbali na watu.

Beth Rehobu

Hili ni jina la mji.

Judges 18:30

Yonathani ... Gershomu ... Musa

Hili ni jina la Mlawi aliyekuwa kuhani wa Mika.

mpaka siku ya uhamisho wa nchi.

Hii ina maana ya kipindi ambacho watu wa Dani wachukuliwa mateka na adui zao. "mpaka siku ambayo adui waliiteka nchi yao"

aliyoifanya

Mika hakuitengeneza miungu lakini fundi aliitengeneza.

Judges 19

Judges 19:1

Katika siku hizo

Hii inaonesha mwanzo wa tukio lingine katika simulizi.

mbali

"mbali na mahali ambapo watu wengi waliishi"

hakuwa mwaminifu kwake

Hii inamaanisha kuwa hakuwa mwaminifu katika mahusiano yao na alianza kulala na wanaume wengine.

Judges 19:3

alimshawishi kukaa

"alizungumza naye ili aamue kukaa"

Judges 19:5

alijiandaa

Mlawi alijiandaa

Jipe nguvu na mkate kidogo

"Mkate" inamaanisha chakula. "Kula chakula kidogo ili upate nguvu ya kusafiri"

Tafadhali uwe tayari kukaa usiku

"Tafadhali kaa tena usiku huu"

Judges 19:7

Jitie nguvu mwenyewe, na usubiri mpaka alasiri

Baba mkwe alitoa mawazo kuwa ajipe nguvu kwa kula chakula. Pia alimuomba asubirie mpaka alasiri ndipo aondoke.

Judges 19:9

sasa mchana unaelekea jioni

"siku inakaribia kuisha" au "jioni inakaribia"

Judges 19:10

hiyo ni Yerusalemu

"Ambayo baadae iliitwa Yerusalemu"

Alikuwa na saruji katika punda

"Aliweka saruji katika punda wake wawili"

Njoo

"Nafikiri"

Tupate kwenda

Hii ina maana ya kupumzika na kusimama mahali katikati ya safari.

Judges 19:12

Tupate kwenda

Hii ina maana ya kupumzika na kusimama mahali katikati ya safari.

Njoo

"Nafikiri"

Judges 19:14

Wakageuka huko

Hii ina maana ya kupumzika na kusimama mahali katikati ya safari.

Naye akaingia

"Naye" inamzungumzia Mlawi lakini pia inazungumzia pamoja na watumishi wake na suria wake.

aliyewaingiza nyumbani kwake

"atakayenikaribisha nyumbani kwake usiku huo"

Judges 19:16

Wabenyamini

Hawa ni uzao wa Benyamini.

Aliinua macho

Hapa mtu aliangalia kwa makini kuona kilichopo pembeni yake. "alitizama juu"

Njia kuu ya mji

Ni sehemu ya soko ambayo watu hukusanyika wakati wa mchana, ni njia kuu za mji.

Judges 19:18

atakayenichukua nyumbani kwake

"atakayenikaribisha nyumbani kwake"

atakayenichukua

Hapa Mlawi alikuwa anamaanisha yeye pamoja na watumishi wake na masuria wake.

na kuna mkate na divai

"na kuna chakula cha kutosha na vinywaji"

yangu na mtumishi wako mwanamke hapa, na kwa kijana huyu pamoja na watumishi wako.

Mlawi anazungumza juu yake pamoja na wengine kama watumishi.

Hatujapungukiwa chochote

"Tuna kila kitu"

Judges 19:20

Usikae

Neno hili linasisitiza kuwa hakutaka Mlawi akae.

Njia kuu

Hii inamaanisha njia kuu za mji pia ni sehemu ya soko ambayo watu hukusanyika wakati wa mchana.

akamleta Mlawi nyumbani kwake

Hii inamaanisha kuwa akamkaribisha Mlawi ashinde nyumbani kwake usiku ule.

Judges 19:22

watu ... walizunguka nyumba

Watu wengi walizunguka pande zote za numba"

Judges 19:24

Angalia

"Sikiliza"

Lakini watu hawakumsikiliza

"watu hawakukipokea kile walichopewa"

huyo mwanamume akamshika yule mwanamke

"Mlawi akamshika mwanamke wake"

Asubuhi

"jua lilipoanza kuchomoza"

huyo mwanamume akamshika yule mwanamke

"mpaka jua lilipochomoza kabisa"

Judges 19:27

Lakini hakujibiwa

Mwanamke hakujibu chochote kwa sababu alikuwa amekufa.

Judges 19:29

Mguu kwa mguu

Mwandishi anatumua maneno haya kuonesha ni kwa namna gani Mlawi aliugawa mwili wa yule mwanamke vipande vipande.

Vipande kumi na mbili

"Vipande 12"

akapeleka vipande kila mahali katika Israeli

"akapeleka kila kipande maeneo tofauti katika Israeli"

Judges 20

Judges 20:1

mtu mmoja

Hii inazungumzia kundi la watu ambalo lipo kama mtu mmoja.

Dani mpaka Beer-sheba

Hii ni nchi kwa ujumla.

Mungu-watu 400,000 waendao kwa miguu

"Mungu na pia askari 400,000 walikuja"

tayari kupigana

"wenye uwezo wa kupigana." Hawakupigana wao kwa wao.

Judges 20:3

Sasa

Mwandishi anatuambia taarifa ya ni kitu gani wanachokifahamu Wabenyamini.

wamepanda Mispa

Mispa ilikuwa juu ya milima.

Ili tulale

"tukae usiku huu"

Judges 20:5

uovu na upumbavu

Huu ni uovu.

Sasa

Hili neno limetumika kuonesha mwisho wa maneno ya Mlawi

toeni maneno na ushauri wenu hapa

"amueni ni nini kifanyike kuhusu jambo hili"

Judges 20:8

kama mmoja

Hii inazungumzia kundi la watu ambalo lipo kama mtu mmoja.

Hakuna hata mmoja wetu atakayeenda hemani kwake ... hakuna hata mmoja wetu atakayerudi nyumbani kwake

Sentensi hizi mbili zina maana moja na hapa zinaonesha msisitizo. "Tutakaa hapa wote"

Lakini sasa

Maneno haya yanaonesha ni kitu gani watu walikuwa wanazungumza.

kama kura inavyotuongoza

Hii inahusisha kuzungusha mawe madogo ili kujua Mungu anataka nini.

Judges 20:10

watu kumi katika mia moja ... mia moja katika elfu ... elfu moja katika elfu kumi

"Watu 10 katika 100 ... 100 katika 1,000 .... 1,000 katika 10,000"

Chakula

"mahitaji"

wakakusanyika juu ya mji

"Wakakusanyika pamoja ili kuuvamia mji"

Judges 20:12

tupate kuwaua

"kuwaua"

sauti ya ndugu zao

"Sauti" inawakilisha ujumbe uliosemwa. "Kile ambacho ndugu yao alikisema"

Judges 20:15

Ishirini na sita elfu

"26,000"

Mia saba

"700"

shoto

Mtu mwenye shoto ni mtu mwenye uwezo wa kutumia mkono wake wa kushoto vizuri kuliko wa kulia.

angeweza kupiga unywele kwa mawe na asikose

"anaweza kupiga kwa kutumia jiwe vizuri"

Judges 20:17

Bila kuhesabu

"bila kujumuishwa"

wakaomba ushauri kutoka kwa Mungu

Wakamuomba Mungu awaambie ni nini cha kufanya"

Judges 20:19

wakahamisha kambi yao karibu na Gibea

"wakatoka na kutazamana na Gibea"

Elfu ishirini na mbili

"22,000"

Judges 20:22

walijitia nguvu wenyewe

Walijipa moyo wenyewe.

wakaunda mstari wa vita

Waisraeli waliandaa mistari yao ya kivita kwa ajili ya siku iliyofuata ya mapigano.

Walitaka mwongozo kutoka kwa Bwana

Kuhani alitegemea mapenzi ya Mungu.

Judges 20:24

Elfu kumi na nane

"18,000"

Judges 20:26

Mbele za Bwana

"kwenye uwepo wa Bwana"

Judges 20:27

wa sababu ya sanduku la agano la Mungu ... akihudumia mbele ya sanduku siku hizo

Mwandishi anatueleza ni kwa namna gani watu waliomba msaada kwa Bwana.

lilikuwapo siku hizo

"lilikuwepo Batheli siku hizo"

akihudumia mbele ya sanduku

"akihudumu kama kuhani mbele ya sanduku"

Wapigeni

"Wapigeni jeshi la Benyamini"

Judges 20:29

Israeli akaweka watu

"Israeli" inamaanisha watu wa Israeli. "Waisraeli"

mahali pa siri

"kwa kuvamia"

Judges 20:31

kupigana na watu

"Kupigana dhidi ya watu wa Israeli"

wakachukuliwa mbali na mji

"Watu wa Israeli wakawachukua nje ya mji"

Walianza kuua baadhi ya watu

"Watu wa Benyamini wakaanza kuwaua baadhi ya watu wa Israeli"

Judges 20:32

kama hapo awali

"kama hapo mwanzo"

Baal-Tamari

Hili ni jina la mji.

Maare-Geba

Hili ni jina la mahali.

Judges 20:34

Elfu kumi

"10,000"

waliochaguliwa

"Askari waliofundishwa vizuri"

msiba ulikuwa karibu nao

"muda si mrefu wataangamizwa kabisa"

Judges 20:36

Wana wa Israeli walikuwa wametoa ardhi kwa Benyamini, kwa kuwa walikuwa wakihesabu watu waliowaweka katika nafasi zilizofichwa nje ya Gibea.

Sentensi hii mpaka mstari wa 41 unaelezea ni kwa namna gani uvamizi ulisababisha Wabenyamini kushindwa.

wametoa ardhi kwa Benyamini

"Waliwaruhusu Wabenyamini kusogea mbele"

walikuwa wakihesabu watu

Waliwaamini watu wao.

Judges 20:39

Taarifa ya jumla:

mstari huu unaelezea ni kwa namna gani uvamizi ulisababisha Wabenyamini kushindwa.

wakageuka kutoka kwenye vita

"wakaondoka vitani"

wanapigwa mbele yetu

"tumewapiga wao"

Judges 20:40

Taarifa ya jumla:

mstari huu unaendelea kuelezea ni kwa namna gani uvamizi ulisababisha Wabenyamini kushindwa.

maafa

"majanga" au "matatizo"

yaliwajia

"yaliwapata"

Judges 20:42

Lakini vita viliwapata

"Lakini hawakuweza kuikimbia vita"

Judges 20:43

Noha

Hili ni jina la mahali.

Nao wakawakanyaga

"wakawaharibu kabisa"

wakawaua

"waliwaua walipokuwa wakikimbia"

Kumi na nane elfu

"18,000"

waliojulikana

"waliopigana kwa ujasiri katika vita"

Judges 20:45

Wakageuka na kukimbia

"Wabenyamini waliobakia waligeuka na kukimbia"

Elfu tano ... elfu mbili

"5,000 ... 2,000"

Gidomu

Hili ni jina la sehemu.

Elfu ishirini na tano

"25,000"

Judges 20:47

Mia sita

"600"

waliwarudia watu wa Benyamini

Watu hawa wa Benyamini ni wale waliokuwepo katika mji.

mji mzima

"mji" inamanisha watu wa mji ule. "kila mtu aliyekuwepo mjini"

katika njia yao

Hii inaelezea kila kitu walichokikuta walipokuwa wakielekea mjini.

Judges 21

Judges 21:1

Sasa watu wa Israeli walikuwa wameahidi huko ... kuolewa na Mbenyamini

Mwandishi anatuambia juu ya ahadi waliyoifanya Waisraeli kabla ya vita na Wabenyamini.

Mbenyamini

Hili ni jina la uzao wa Benyamini.

Kwa nini, Bwana, Mungu wa Israeli, amefanya jambo hili kwa Waisraeli, kwamba moja ya makabila yetu linapotea leo?

Waisraeli walitumia swali hili kuelezea ni kwa namna gani walikuwa na huzuni kubwa.

Judges 21:4

Watu wa Israeli wakasema, "Ni nani kati ya kabila zote za Israeli hawakuja katika mkutano wa Bwana?

Watu wanaukumbuka mkutano wa Waisraeli kule Mispa kabla ya kuwakamata Wabenyamini.

Kwa kuwa walikuwa wamefanya ahadi muhimu juu ya mtu yeyote ambaye hakuja kwa Bwana huko Mispa. Wakasema, "Hakika yeye atauawa."

Mwandishi anaeleza ahadi ambayo Waisraeli waliifanya huko Mispa kabla hawajakamatwa na Wabenyamini.

Judges 21:6

ndugu yao Benyamini.

"ndugu yao Benyamini" inamaanisha uzao uliobaki wa Benjamini.

kabila moja limekatiliwa mbali kutoka Israeli

Kuharibiwa kwa kabila la Benyamini kunafananishwa na kukatiliwa mbali kutoka katika Israeli.

Ni nani atakayewapa wale walioachwa wake, kwa kuwa tumeahidi kwa Bwana kwamba hatuwezi kuwaruhusu yeyote kati yao aoe binti zetu?

Waisraeli walitaka kuwapa wake Wabenyamini waliosalia lakini ahadi waliyoiweka Mispa iliwazuia kufanya hivyo.

Judges 21:8

Jabeshi-Gileadi

Hili ni jina la mji.

watu walipokuwa wamepangwa kwa utaratibu

"watu waliokuwa wamekusanyika huko Mispa walikuwa wamepangwa"

hakuna hata mmoja wa wenyeji wa Yabeshi Gileadi

"hakuna hata mmoja wa uzao wa Yabeshi Gileadi aliyekuwepo Mispa"

Kumi na mbili elfu

"12,000"

Waueni, hata wanawake na watoto.

Mistari inayofuata inaweka mipaka juu ya maelekezo haya.

Judges 21:11

Yabeshi-gileadi

Hili ni jina la mji.

kulala na mwanaume

Hiki ni kitendo cha kuwa na uhusiano wa kimapenzi.

Wanawake mia nne

"wanawake 400"

Judges 21:13

walikuwa wanawapa amani

"Walitaka kufanya amani pamoja nao"

Yabeshi Gileadi

Hili ni jina la mji.

hapakuwa na wanawake wa kutosha kwa wote

Kulikuwa na Wabenyamini mia sita na wanawake kutoka Yabeshi Gileadi walikuwa mia nne.

alifanya mgawanyiko kati ya makabila ya Israeli.

"alisababisha makabila ya Israeli yasiwe na umoja"

Judges 21:16

Mbenyamini

Huu ni uzao wa Benyamini.

wanawake wa Benyamini wameuawa

"tumewauwa wanawake wote wa Benyamini"

Lazima kuwe na urithi ... lisiharibiwe kutoka Israeli.

Waisraeli wanaongeza chunvi tuu. Tayari walishawapa Wabenyamini wake mia nne hivyo kabila halitaharibiwa moja kwa moja.

Judges 21:18

mke kwa Benyamini

"mke kwa watu wa Benyamini"

ambayo ni kaskazini ya Betheli, mashariki ya barabara inayopanda kutoka Betheli hadi Shekemu, na kusini mwa Lebona

Haya ni maelezo yanayotolewa ili kumuwezesha msomaji kuelewa ulipo mji wa Shilo.

Lebona

Hili ni jina la mji.

Judges 21:20

kila mmoja wenu anapaswa kunyakua mke ... rudi kwenye nchi ya Benyamini

"Kila mmoja wenu anapaswa kuchukua binti toka Shilo na kisha kuondoka nao kuwapeleka kwenye nchi ya Benyamini na kuwa wake zenu"

Judges 21:22

Tupeni neema

"tuonesheni upole sisi pamoja na watu wa Benyamini"

kwa sababu hatukupata wake kwa kila mtu wakati wa vita

"kwa sababu hatukupata wake kwa kila mtu wakati wa vita na Yabeshi Gileadi"

ninyi hamna hatia ... hamkuwapa wao binti zenu

Hapa wanaambiwa watu wa Shilo. Hawakuwatoa binti zao kwa watu wa Benyamini na hivyo hawakuvunja ahadi yao ya kutokufanya hivyo.

Judges 21:23

idadi ya wake waliowahitaji

Mke mmoja kwa kila Wabenyamini mia mbili ambao hawakupewa wake kutoka Yabeshi Gileadi.

Judges 21:25

hapakuwa na mfalme huko Israeli

"Bado Israeli haikuwa na mfalme"

yaliyo sawa machoni pake mwenyewe

"macho" inawakilisha mawazo ya mtu au fikra zake. "aliyoyaona kuwa ni sawa"

Ruth 1

Ruth 1:1

Ikatokea

"ilikuwa"

wakati waamuzi walipo tawala

"kipindi waamuzi waliongoza Israeli"

katika nchi

"katika nchi ya Israeli"

mwanaume mmoja

"mwanaume" Hii ni namna ya kukaribisha mtu kwenye stori.

Ruth 1:3

aliachwa na wanae wawili

"Naomi alikuwa na wanae wawiili"

akachukuwa wake

"akaoa wanawake"

kutoka wanawake wa Moabu

Wana wa Naomi walioa wanawake kutoka kabila la Moabu

jina la mmoja

"jina la mmoja wa wanawake"

Ruth 1:6

alisikia katika nchi ya Moabu

"wakati Naomi anaishi na Moabu alisikia"

Yahweh

Hili ni jina la Mungu alilo lirihidhisha kwa watu wa Agano la Kale.

alisaidia watu wake kwenye shida

Mungu aliona mahitaji yao na kutoa mavuno mazuri kwa ajili yao

Ruth 1:8

kila mmoja wenu

Naomi alikuwa anaongelea watu wawili

nyumba ya mama yenu

"kwa nyumba ya mama zenu"

alionyesha ukarimu

"alirihidhisha uaminifu"

kwa wafu

"kwa waume zenu, waliyo kufa"

kwenye nyumba ya mume mwingine

na waume zao wapya, sio mume wa mtu mwingine

Ruth 1:11

kwanini uende na mimi?

Hili ni swali lisilo itaji jibu

Bado ni wana wa kiume tumboni mwangu , ili kwamba wawe waume zenu?

Naomi anatumia hili swali kusema kuwa hana tena wana wa kiume wa kuwaoa

mzee sana kuwa na mume

Hii yaweza andikwa kwa uwazi zaidi

Ruth 1:14

wakainua sauti zao na kulia

Hii ina maana walilia kwa uchungu

sikia

"Sikia" hapa ina maana ya "chukuwa tahadhari"

Ruth 1:16

una ishi wapi

"wapi unaishi"

watu wako watakuwa watu wangu

Ruthi anaeleza kuhusu watu wa Naomi, Waisraeli

Utakapo kufa nitakufa

Hii ina onyesha matamanio ya Ruthi ya kuishi maisha yake yote sehemu moja na Naomi

Ruth 1:19

ikatokea

"ikaja kutokea"

mji wote

"kila mtu katika mji"

Ruth 1:22

Kwaiyo Naomi na Ruthi

Hii ina hitimisha

Ruth 2

Ruth 2:1

Sasa mume wa Naomi

Hii ina tambulisha taarifa kabla ya stori kuendelea.

tajiri, wanaume mwenye ushawishi

"mtu maarufu, tajiri"

Ruthi, Wamoabu

Hapa stori inaendelea.

Wamoabu

Hii ni njia ingine ya kusema mwanamke alitoka nchi au kabila la Moabu

Ruth 2:3

Tazama, Boazi

Neno "tazama" lina ashiria tukio muhimu Boazi akija shambani

akatoka Bethilehemu

Mashamba yalikuwa ya yajatajwa umbali na Bethilehemu

kukubariki

"kukupa vitu vizuri"

Ruth 2:5

Huyu mwanamke mdogo ni wa mwanamme gani?

Maana zinazo wezekana ni 1) Boazi alikuwa anauliza kuhusu mume wa Ruthi au 2) Boazi alikuwa anauliza wazazi au walezi

usimamizi

"muhusika wa"

Ruth 2:8

Una nisikiliza mimi, binti yangu

Hii yaweza andikwa kama amri

binti yangu

Hii ilikuwa namna ya ukarimu ya kumtaja mwanamke

Eka macho yako shambani

Macho yanawakilisha kutizama kitu

Ruth 2:10

akainama mbele za Boazi, akishika kichwa chake kwenye ardhi

Haya ni matendo ya heshima na hofu.

kwanini nimepata kibali

Ruthi anauliza swali

mgeni

Ruthi aliweka uaminifu wake kwa Mungu wa Israeli sirini, lakini alijulikana hadharani kama Mmoabu

Imeletwa kwangu

Hii yaweza andikwa kama kitenzi tendaji.

Ruth 2:13

Acha nipate kibali machoni pako

Hii yaeleza kuomba baraka

Ruth 2:14

Wakati wa chakula

Hii ina maana ya mchana

Ruth 2:15

Alipo inuka kukusanya nafaka, Boazi aliamuru vijana wake

Katika muktadha wa amri, inawezekana Ruthi alikuwa mbali sana na maelekezo ya Boazi

Alipo inuka

"Alipo inuka"

usimkeme

"usimsababishie aibu"

Ruth 2:17

maskio ya nafaka

Hii ina maana ya vitu vinavyo liwa vya nafaka

Akainua juu na kwenda mjini

Ina ashiriwa kwamba Ruthi alibeba nafaka nyumbani

mama mkwe wake aliona

Naomi aliona

Ruth 2:19

yeye abarikiwe na Yahweh

Naomi ana muuliza Mungu kumpa thawabu Boazi kwa ukarimu wake kwa Ruthi na yeye.

kwa waliyo hai

"kwa watu wanao ishi"

wafu

"watu waliyo kufa"

Ruth 2:21

Hakika, alisema kwangu

"Ata aliniambia"

kuwa karibu na vijana wangu

Boazi alikuwa anaongelea ulinzi wa kimwili vijana wake wanaweza mpa

toka na

"fanya na"

Ruth 2:23

alikuwa karibu

Ruthi alifanya kazi shambani mwa Boazi na wafanya kazi wake mchana, ili awe salama

aliishi na mama mkwe wake

Ruthi alienda kwa Naomi kulala usiku

Ruth 3

Ruth 3:1

mama mkwe

Naomi ni mama wa mume wa Ruthi aliye kufa

Binti yangu

Ruthi alikuwa binti wa Naomi kwa kumuoa mwanae na kwa matendo yake baadae kwa kumjali Naomi baada ya kurudi Bethilehemu

wafanya kazi wa kike uliyo kuwa nao

"wafanya kazi wa kike umekuwa ukifanya nao kazi"

sio ndugu yetu?

Naomi labda alitumia hili swali kumkumbusha Ruthi kitu

Angalia

Hii ina maana kuwa maelezo ya fuatayo ni muhimu sana

Ruth 3:3

jipake mafuta mwenyewe

Ina inazekana ni kujipaka mafuta ya kunukia mwilini, kama wanawake wanavyo jipaka marashi leo

lala chini hapo

"lala kwenye miguu yake"

Ruth 3:6

moyo wake ulifurahi

"aliridhika"

alikuja tarajibu

"alinyata ndani"

akafunua miguu yake

"aliondoa shuka miguuni mwake"

Ruth 3:8

Ikaja kuwa kwamba

Haya maneno yanatumika kuonyesha jambo muhimu katika stori.

usiku wa manane

"katikati ya usiku"

Aligeuka

Aliangalia nini kimemgusa

mwanamke alikuwa amelala miguuni mwake

Mwanamke alikuwa Ruthi, lakini Boazi hakuweza kumtambua gizani

Ruth 3:10

binti yangu

Boazi alitumia msemo huu kama ishara ya heshima kwa Ruthi kama mwanamke mdogo

ukarimu mwishoni kuliko mwanzoni

"ukarimu zaidi sasa kuliko kabla"

ukarimu mwishon

Hii ina eleza kuwa Ruthi anamuomba Boazi kumuoa

Ruth 3:12

kama hatafanya jukumu la ndugu

"kama hatamuoa ndugu wa mjane wake na kuzaa watoto kwa ndugu yake aliyo kufa

kwa maisha

"hakika kama Yahweh aishvyo"

Ruth 3:14

amelala miguuni mwake

Ruthi alilala miguuni mwa Boazi. Hawaku fanya mapenzi

kabla ya mtu yeyote kumtambua mwenzake

Wakati huu wa siku unaweza elezwa kama giza

kuweka mzigo juu yake

Kiasi cha nafaka kilikuwa kikubwa hadi Ruthi alihitaji msaada kubeba

Ruth 3:16

Ulifanyaje binti yangu?

Alicho maanisha Ruthi kwa hili swali la weza andikwa wazi zaidi.

yote mwanaume aliyo fanya

"yote Boazi aliyo fanya"

Usiende mtupu

"usiende mikono mitupu"

Ruth 4

Ruth 4:1

lango

"lango la mji" Hili lilikuwa mwingilio wa mji wa ukuta wa Bethilehemu.

ndugu wa karibu

Huyu alikuwa ndugu wa karibu wa Elimeleki

wazee wa mji

"viongozi wa mji"

Ruth 4:3

katika uwepo wa

Hii ilifanya muamala wa kisheria na wa kufunga

kumboa

Hii ili maanisha kununua ardhi ili kuweka ndani ya familia yao

Niko baada yako

Boazi alikuwa ndugu anaye fuata kununua ardhi

Ruth 4:5

Siku utakayo nunua ... lazima pia

Boazi anatumia huu msemo kutambulisha ndugu zake majukumu ya ziada atakayo kuwa nayo atakapo nunua ardhi

kutoka nchi ya Naomi

"kutoka kwenye umiliki wa Naomi"

lazima pia umchukuwe Ruthi

"lazima umuoe Ruthi"

Ruthi ... mke kwa mwanaume aliye kufa

"Ruthi ... mjane wa mwana wa Elimeleki"

Ruth 4:7

Sasa hii ilikuwa desturi

Mwandishi wa kitabu anaelezea desturi za kubadilishana kipindi cha Ruthi

wakati wa awali

"kipindi cha nyuma"

kiatu

"ndala"

jirani yake

Hii yaeleza mtu aliye kuwa anafanya naye makubaliano.

Ruth 4:9

kwa wazee na watu wote

Hii yaeleza watu wote waliyo kuwepo sehemu hiyo, sio kila mtu mjini

yote yaliyo kuwa ya Elimeleki na yote yaliyo kuwa ya Kilioni na Mahaloni

Hii yaeleza mali za mume wa Naomi aliye kufa na wanae

kutoka mkono wa Naomi

Mkono wa Naomi una wakilisha Naomi

Ruth 4:11

watu waliyo kuwa langoni

"watu waliyo kuwa wanakutana pamoja langoni"

jenga nyumba ya Israeli

"kuzaa watoto wengi waliyo kuwa taifa la Israeli"

kama Raheli na Lea

Hawa walkuwa wake wawili wa Yakobo, ambaye jina lake lilibadilishwa kuwa Israeli

nyumba yako iwe kama

Mungu kwa utele alimbariki Yuda kupitia mwanae Perezi.

Ruth 4:13

Boazi akamchukuwa Ruthi

"Boazi alimuoa Ruthi"

Akalala naye

"Akafanya naye mapenzi"

ambaye hajakuacha leo bila ndugu wa karibu

"ambaye leo amekupatia ndugu mzuri wa karibu"

Ruth 4:16

Naomi akachukuwa mtoto

Hii ya husu Naomi kushikilia mtoto.

akamueka kifuani

Hii sentensi ya upendo kwa mtoto

mwana wa kiume amezaliwa kwa Naomi

Ilieleweka kwamba mtoto alikuwa mjukuu wa Naomi, sio mtoto wake wa kimwili

baba wa Daudi

"mtoto wa mfalme Daudi"

Ruth 4:18

wazao wa Perezi

"wazao waliyo rithi." Mwandishi anaendelea kuorodhesha familia ya Perezi

1 Samuel 1

1 Samuel 1:1

Rama Msufi

Hili ni jina la kijiji kidogo kilichokuwa kilometa nane mashariki mwa Yerusalemu.

Elikana ... Yerohamu ... Elihu ... Tohu ... Sufu

Haya ni majina ya wanaume.

Penina

Hili ni jina la mwanamke.

1 Samuel 1:3

Mtu huyu

"Mtu huyu" inamuelezea Elikana.

Eli, Hofni na Finehasi

Haya ni majina ya wanaume.

1 Samuel 1:5

Hana

Hili ni jina la mwanamke.

Hasimu wake alimchokoza sana.

Mke mwingine alimdhihaki na kumuaibisha Hana.

Amelifunga tumbo lake

"amemfanya kuwa mgumba" au "amezuia kupata mimba."

1 Samuel 1:7

Hasimu wake

Huyu ni Penina mke mwingine wa Elikana. Hasimu ni mtu anayeshindana na mtu mwingine. Penina alikuwa anashindana na Hana na kujaribu kumfanya Elikana ampende yeye zaidi.

"Hana, kwa nini unalia? Kwa nini huli chakula? Kwa nini una huzuni moyoni mwako? Mimi si bora kwako kuliko wana kumi?

Swahi hili linaweza kutafsiriwa kama sentensi isemayo, "Hana usilie. Yakupasa ule na moyo wako ufurahi kwa sababu mimi ni bora kuliko wana kumi!"

Kuliko wana kumi

Elikana alitumia maneno haya kusisitiza kouonesha ni kwa kiasi gani Hana alikuwa na umuhimu kwake.

1 Samuel 1:9

Maelezo ya jumla:

Hana anaanza kuomba kwa Bwana na Eli anamtazama.

Hana alinyanyuka

Taarifa hii yaweza kuwa na maana ya kuwa Hema ya Hana ilikuwa karibu na maskani au alitembea toka kwenye Hema yake mpaka maskani kuomba. "Hana alinyanyuka na akaenda kwenye nyumba ya Bwana kuomba."

Wakati huo Eli kuhani

Hapa mwandishi anatuambia kuhusu mtu mwingine katika simulizi. Mtu huyu ni kuhani Eli.

Hekalu la Bwana.

Hekalu ni Hema lakini ilikuwa ni sehemu ambayo watu hutumia kuabudu hivyo ni vyema kuitafsiri kama Hekalu.

Alikuwa na uchungu sana.

Alikuwa ana katika matatizo makubwa au katika kuomboleza kwa sababu ya kutokuwa na mtoto na kuonewa na Penina mke mwingine wa Elikana.

1 Samuel 1:11

Taarifa ya jumla:

Maombi ya Hana kwa Bwana yanaendelea.

teso la mjakazi wako

Hii yaweza kuwa na maana ya 1) Hana kutokuwa na uwezo wa kuwa mjamzito au 2) namna ambavyo Penina anamdhihaki.

Unikumbuke

Hili ni ombi maalumu kwa Mungu. Mungu anajua yanayompata Hana hajasahau.

Usimsahau mjakazi wako

Hii ina maana sawa na "unikumbuke."

1 Samuel 1:12

Eli alimtazama

Eli alikuwa kuhani mkuu, hivyo alikuwa ndani ya hema ya Mungu na akiwaongoza.

1 Samuel 1:15

mimi ni mwanamke mwenye roho ya huzuni

"Mimi ni mwanamke mwenye huzuni sana"

nimemimina nafsi yangu mbele za Bwana

"Namwambia Bwana hisia zangu za ndani"

mjakazi wako

Hana anajizungumzia mwenyewe kwa kuonesha unyenyekevu.

nimekuwa nikiongea kutokana na maumivu na masikitiko yangu

Hii ni namna nyingine ya kusema kuwa ana "roho ya huzuni" Hii inaweza kutafsiriwa kama "Ninazungumza kwa sababu nina huzuni sana na hasimu wangu ananidhihaki sana"

maumivu na masikitiko

Maneno haya yote yanaonesha kuwa Hana amekosa raha na anahuzuni kwa sababu ya kudhihakiwa na Hasimu wake.

Maumivu

Haya ni mambo ambayo Penina alimfanyia ya kumuumiza.

Masikitiko

Hana anaelezea maumivu na aibu anayoipata kwa sababu ya namna Hana anavyomfanyia.

1 Samuel 1:17

Kisha Eli akamjibu

Eli akiliwa kuhani mkuu aliyeishi katika maskani.

Mjakazi wako

Hana anajizungumzia mwenyewe kwa kuonesha unyenyekevu na heshima kwa Eli kuhani mkuu.

na kula; uso wake

Hapa "uso wke" inamaanisha Hana mwenyewe.

1 Samuel 1:19

akamkumbuka

Mungu alijua yaliyokuwa yanampata Hana hakusahau.

Hana akapata mimba

"Hana akawa mjamzito?

1 Samuel 1:21

Nyumba yake

"Nyumba" inamaanisha watu wanaoishi ndani ya nyumba. "Familia yake"

Aache kunyonya

Kuacha kunywa maziwa na kuanza kula vyakula vyenye kimimimika.

ahudhurie mbele za BWANA na akae huko daima

Hana alimuahidi Mungu kuwa atamruhusu Samweli aishi na kufanyakazi na Eli katika hekalu.

kumnyonyesha mtoto

"kumpa mtoto wake maziwa"

1 Samuel 1:24

Efa

Efa ni kama lita 22 za unga.

Chupa

Mvinyo uliwekwa katika ngozi ya wanyama na sio chupa chuma.

1 Samuel 1:26

Akasema, "Ee bwana wangu! Kama uishivyo, bwana wangu

"Kama uishivyo" inaonesha kuwa Hana amekuwa mkweli na mwaminifu. "bwana ninachokwenda kukwambia ni kweli"

amenijibu ombi la dua yangu nililomwomba

Hana anazungumza juu ya dua kama kitu ambacho mtu anaweza kumpa mtu mwingine pia anazungumza juu ya dua kama jibu la ombi lake. Hii inaweza kutafsiriwa kama "amekubali kunifanyia nilichomuomba anifanyie"

Alimwabudu Bwana

Hii inamuelezea Elikana lakini tafsiri zingine humuelezea Elikana na familia yake.

nimempa BWANA

Hii inaweza kutafsiriwa kama "Nimemkopesha kwa Bwana"

1 Samuel 2

1 Samuel 2:1

Taarifa ya jumla:

Hana anamwimbia Bwana wimbo.

Moyo wangu wamtukuza

"nina furaha kubwa"

Katika Bwana.

"Kwa sababu ya Bwana" au "kwa sababu Bwana ni mkuu"

Pembe yangu imejulikana

Pembe ni ishara ya nguvu. "Sasa nina nguvu."

1 Samuel 2:2

Taarifa ya jumla:

Hana anaendelea kumwimbia Bwana.

hakuna mwamba kama Mungu wetu.

Hii ni namna nyingine ya kusema kuwa Mungu ni mwenye nguvu na mwaminifu.

Mwamba

Huu ni mwamba mkubwa ambao unaweza kujificha nyuma yake na kuwa juu ya adui.

1 Samuel 2:3

Taarifa ya jumla:

Hana anaendelea kumwimbia Bwana wimbo. Anazungumza kama vile watu wengine wanamsikiliza.

Hakuna majivuno

"hakuna maneno ya majivuno"

Kwa yeye matendo hupimwa

Hii inaweza kuandikwa kama "Yeye anapima matendo ya watu"

Pinde za mashujaa zimevunjika

Yaweza kuwa na maana ya 1) pinde zenyewe zimevunjika au 2) watu waliobeba pinde wamekatazwa kufanya. "Watu wenye ushujaa wamenyimwa kufanya"

Pinde za mashujaa zimevunjika

Hii inaweza kutafsiriwa kama "Bwana amezivunja pinde za mashujaa" au "Bwana amewafanya hata watu wenye nguvu kuwa dhaifu"

wale wanaojikwaa hujivika nguvu kama mshipi

Hii inamaanisha kuwa hawatajikwaa tena bali nguvu zao zitakuwa pamoja nao kama mshipi uliobana. "Bali atawafanya waliojikwaa kuwa na nguvu"

kujivika ... mshipi

Hiki ni kitendo cha kuvaa kitu kuzunguka kiuno na kujiandaa na kazi.

1 Samuel 2:5

Taarifa ya jumla:

Hana anaendelea kumwimbia Bwana.

amezaa saba

amezaa watoto saba

amenyong'onyea

kutokuwa na nguvu na kuwa mpweke.

1 Samuel 2:6

Taarifa ya jumla:

Hana anaendelea kumwimbia Bwana.

Bwana huua ... huuisha... hushusha... huleta juu ... humfanya mtu masikini ... mwingine tajiri ... hunyenyekeza ... hukweza.

Bwana ndiye mwenye mamlaka na kila kitu.

1 Samuel 2:8

Taarifa ya jumla:

Hana anaendelea kumwimbia Bwana.

Wahitaji

Watu wasiokuwa na kitu wanachohitaji.

toka mavumbini ... toka jalalani

Hii inaonesha hali ya watu wa daraja la chini katika jamii.

1 Samuel 2:9

Taarifa ya jumla:

Hana anaendelea kumwimbia Bwana.

anazilinda nyayo za watu wake waaminifu

"nyayo" inamaana ya njia za mtu anazopita, ambayo ni maisha ambayo mtu ameamua kuishi. "anawalinda watu wake waaminifu wasifanye maamuzi mabaya" au "anawasaidia watu wake waaminifu kufanya maamuzi ya busara"

waovu watanyamazishwa gizani

Hii ni njia ya busara ya kusemma kuwa Bwana atawaua watu waovu.

waovu watanyamazishwa

Neno "kunyamazishwa" inamaana ya "kumfanya anyamaze" Bwana atawafanya wanyamaze.

kwa nguvu

"kwa sababu ana nguvu"

1 Samuel 2:10

Taarifa ya jumla:

Hana anaendelea kumwimbia Bwana.

Wale wampingao BWANA watavunjwa

"Bwana atawavunja wale wanaompinga"

Kuvunjwa vipande vipanade

Hii inamaana ya "watashindwa"

miisho ya dunia

Neno hili linamaana ya kila sehemu. "dunia nzima"

kuinua pembe ya mtiwa mafuta wake

Pembe ni ishara ya nguvu. " viongozi aliowachagua atawapa nguvu zaidi ya adui zao"

mtiwa mafuta wake

Hii inaweza kutafsiriwa kama "aliyetiwa mafuta" Mafuta ilikuwa ishara kuwa Bwana amemchagua mtu huyo ambaye amempaka mafuta ili aongoze juu ya watu.

1 Samuel 2:12

Taarifa ya jumla:

Watu walipokuwa wakitoa dhabihu za wanyama, walichoma mafuta ya mnyama kwanza kisha walichemsha nyama na kula.

Hawakumjua Bwana

Hawakumsikiliza Bwana au kumtii.

Desturi

Desturi ni tendoambalo watu hulifanya mara kwa mara.

sufuria ... birika ... chombo ... chungu

Hivi ni vyombo vinavyotumika kupikia chakula.

sufuria

Ni chombo kidogo cha chuma kwa ajili ya kuchemshia.

Birika

Ni chombo kikubwa kizito cha chuma kwa ajili ya kuchemshia.

chombo

Ni chombo kikubwa kizito cha chuma kwa ajili ya kuchemshia.

chungu

Ni chombo cha udongo kwa ajili ya kupikia

1 Samuel 2:15

Taarifa ya jumla:

Watu walipokuwa wakitoa dhabihu za wanyama, walichoma mafuta ya mnyama kwanza kisha walichemsha nyama na kula.

mbaya, kabla

"Walifanya jambo bata zaidi kuliko hapo mwanzo."

Walichoma

"Mtu aliyetoa dhabihu alichukua dhabihu yake akaipeleka kwa kuhani kisha kuhani akaichoma"

Nipe nyama ya kuchoma kwa ajili ya kuhani

"Nipe mimi nyama ili nikampe kuhani aichome"

Kuchoma

Kupika juu ya moto

Kuchemsha

Kupika ndani ya maji

Mbichi

Haijapikwa

waliidharau dhabihu ya BWANA

Vijana hawakupenda maelekezo ya Bwana kuhusu dhabihu na hawakujali.

1 Samuel 2:20

sababu ya ahadi yake aliyoitoa kwa Bwana

Hana alimuomba Bwana ampe mtoto na aliahidi kuwa atamtoa mtoto amtumikie katika hekalu.

Mbele za Bwana

Mahali ambapo Bwana atamuona na Samweli atajifunza mambo ya Bwana.

1 Samuel 2:22

Kwa nini mnafanya mambo hayo?

Swali hili linaweza kutafsiriwa kama "Ni vibaya kufanya mambo haya!"

1 Samuel 2:25

ni nani atakayemtetea mtu huyo?

Swahi hili linaweza kiutafsiriwa kama sentensi "Hakuna mtu atakayemtetea mtu huyo."

kumtetea mtu huyo

"Kumuomba Bwana rehema juu ya mtu huyo"

Sauti ya baba yao

Sauti inawakilisha mtu. "Aliyoyasema baba yao"

1 Samuel 2:27

Mtu wa Mungu

Mara nyingi humaanisha nabii wa Bwana. "Mtu anayesikia na kusema maneno toka kwa Mungu"

Je, sikujifunua mwenyewe ... nyumba?

Swali hili linaweza kutafsiriwa kama sentensi "Mnapaswa kujua kuwa nilijifunua mwenyewe ... nyumba."

nyumba ya baba zako

"Nyumba" inamaanisha watu wanaokaa ndani ya nyumba. "Famila ya baba zako"

Baba yako

Haruni

apande madhabahuni kwangu, na kufukiza uvumba

Hii inamaana ya kutoa sadaka kwa Bwana.

kuvaa kanzu ya naivera mbele yangu

Maneno "kuvaa kanzu ya naivera" inaonesha kazi ya makuhani wanaovaa naivera. "Kufanya niliyowaamuru makuhani wafanye"

1 Samuel 2:29

Kwanini basi, unaidharau dhabihu yangu ... ninapoishi?

"Hampaswi kudharau dhabihu yangu ... mahali ninapoishi."

Mahali ninapoishi

"Mahali ambapo watu wangu huniletea dhabihu"

kujinenepesha ninyi wenyewe kwa uzuri wa kila sadaka

Sehemu nzuri ya sadaka ilitakiwa kuchomwa kama sadaka kwa Bwana lakini makuhali walikuwa wanakula.

Nyumba ya baba yako

"Nyumba" inamaanisha watu wanaokaa ndani ya nyumba. "Famila ya baba zako"

yawapasa kwenda mbele zangu

"Kuishi kwa kunitii mimi"

Mambo haya yapishe mbali nami nisifanye hivi

"Sitaruhusu familia yako wanitumikie daima"

wanaonidharau mimi hawatakuwa na thamani.

"Hawatakuwa na thamani hao wanaonidharau" au "Nitawadharau hao wanaonidharau"

1 Samuel 2:31

Tazama

"Sikiliza kwa makini ninayotaka kuzungumza" au "ninayotaka kuzungumza ni ya muhimu sana"

Nitaondoa nguvu zako na nguvu za nyumba za baba yako

"Nitakuua wewe pamoja na vijana wtote wenye nguvu wakiume wa uzao wa familia yako"

Nitasababisha macho yenu yashindwe

"nitasababisha mshinwe kuona" au "ntasababisha muwe vipofu"

1 Samuel 2:34

nitamwinua ... kuhani wangu mwaminifu

"Nitamfanya mtu awe kuhani"

kwa ajili yangu

"anitumikie mimi"

kile kilichomo moyoni mwangu na nafisini mwangu

"Ninachotaka afanye na nitakachomwambia afanye"

Nitamjengea nyumba madhubuti

Hapa "nyumba" imeelezewa kama "uzao." Nitahakikisha kuwa uzao wake unatumika kama kuhani mkuu.

1 Samuel 2:36

Yeye

Kuhani mwaminifu atakayeinuliwa na Bwana.

ili niweze kula kipande cha mkate

"Kipande cha mkate kimetumika kama "chakula." Ili niweze kula.

1 Samuel 3

1 Samuel 3:1

Neno la Bwana halikupatikana kwa wimngi

"Bwana hakuzungumza mara kwa mara na watu"

Taa ya Mungu

Huu ni mshumaa wa saba uliopo mahali patakatifu pa maskani unaowaka kila siku mchana na usiku mpaka unapokwisha.

Hekalu la Bwana.

Hekalu ni Hema lakini ilikuwa ni sehemu ambayo watu hutumia kuabudu hivyo ni vyema kuitafsiri kama Hekalu.

1 Samuel 3:5

Mwanangu

Eli hakuwa baba yake na Samweli. Eli anazungumza kama vile yeye ndiye baba yake na Samweli kuonesha kuwa hajamkasirikia lakini Samweli anapaswa kumsikiliza.

1 Samuel 3:7

wala hakuwahi kupata ujumbe wowote kutoka kwa BWANA ukifunuliwa kwake

"Wala Bwana hakukufunua ujumbe wowote kwake"

1 Samuel 3:9

Mtumishi wako ana

Eli alimwambia Samweli azungumze na Bwana ili Samweli aoneshe heshima kwa Bwana.

1 Samuel 3:10

Bwana alikuja na kusimama

Hii inaweza kuwa na maana ya 1) Bwana alimtokea Samweli na kusimama mbele yake au 2) Bwana alifanya uwepo wake uonekane kwa Samweli.

Mtumishi wako ana

Samweli anazungumza na Bwana na kuonesha heshima.

ambalo masikio ya kila mmoja yakisikia yatashtuka

Hapa "masikio ... yatashtuka" inamaanisha kuwa kila mtu atashituka kutokana na kitu atakachokisikia.

Kushtuka

Kuhisi kama vile mtu anakuchoma na kitu chenye ncha au kushtuka kwa sababu mtu amepiga kibao sehemu fulani ya mwili.

1 Samuel 3:12

kutoka mwanzo hadi mwisho

"karibu kila kitu"

walijiletea laana juu yao wenyewe

"walifanya mambo ambayo Bwana alisema kuwa atawaadhibu wanaofanya mambo hayo"

dhambi za nyumba yake hazitasahehewa kwa dhabihu au kwa sadaka

"Hakuna dhabihu au sadaka ambayo mtu ataitoa na kufanya dhambi za nyumba hii zisamehewe"

Dhambi za nyumba yake

"dhambi ambazo watu wa nyumba yake wamefanya"

1 Samuel 3:15

Nyumba ya Bwana

"nyumba" ni hema lakini hapa imetafsiriwa kama nyumba.

Mwanangu

Eli hakuwa baba yake na Samweli. Eli anazungumza kama vile yeye ndiye baba yake na Samweli kuonesha kuwa hajamkasirikia lakini Samweli anapaswa kumsikiliza.

1 Samuel 3:17

Neno alilosema

"ujumbe alioutoa Bwana"

Mungu akutendee hivyo na kukuzidishia

Hii inaonesha ni kwa namna gani Eli alikuwa anasisitiza "Mungu akuadhibu sawasawa na alivyosema ataniadhibu na hata zaidi"

1 Samuel 3:19

hakuacha kutimiza maneno yake ya unabii

"alifanya mambo yote aliyoyafanyia unabii kutimia"

Israeli yote

Watu wote wa Israeli.

tokea Dani hadi Beersheba

"sehemu zote za nchi" au "toka mwisho wa nchi hadi upande mwingine"

Samweli aliteuliwa

Bwana alimteua

1 Samuel 4

1 Samuel 4:1

Ebenezeri ... Afeki

Haya ni majina ya mahali.

Israeli ilishindwa na Wafilisti

"Wafilisti waliwashinda Waisraeli na kuwaua."

watu wapatao elfu nne

Idadi hii sio kamili yaweza kuwa zaidi ya watu elfu nne au pungufu ya watu elfu nne, hii inaonesha kuwa hakukuwa na idadi kamili.

1 Samuel 4:3

Watu

Askari waliokuwa wakipigani vitani.

Kwa nini BWANA ametushinda leo mbele ya Wafilisti? Hebu tulilete

Wazee hawakujua kwa nini Bwana amewashinda lakini walifikiri kuwa wanafahamu namna ya kufanya ili hali hiyo isijirudie tena.

akaaye juu ya makerubi

Japokuwa Bwana yupo kila mahali alijionesha mwenyewe kwa wana wa Israeli juu ya makerubi waliokuwepo juu ya sanduku.

Finehasi

Finehasi huyu hakuwa mjukuu wa Haruni katika Kutoka na Hesabu.

Walikuwepo huko

Walikuwepo Shilo.

1 Samuel 4:5

Sanduku la agano lilipokuja kambini

"watu walipolipeleka sanduku la agano la Bwana katika kambi" "Watu waliokuwepo pamoja na Hofini na Finehasi walilibeba sanduku la agano la Bwana na kulipeleka kambini."

Sanduku la Bwana lilifika kambini

"Watu walilipeleka sanduku la Bwana kambini"

1 Samuel 4:7

Wakasema ... wakasema

Wafilisti walisemezana wao kwa wao. "walisemezana wao kwa wao... walisemezana wao kwa wao"

mungu ameingia

Wafilisti waliabudu miungu mingi hivyo waliamini kuwa moja kati ya miungu ambayo hawakuiabudu alikuja kambini. Walikuwa wakizungumza juu ya Mungu wa Israeli. Baadhi ya tafsiri zinasomeka "Mungu ameingia"

miungu yenye nguvu ... miungu inayoshambulia

Kwa sababu neno mungu (au Mungu) katika sura ya 4:7 ni umoja tafsiri nyingi zimeandika "mungu mwenye nguvu ... mungu anayeshambulia" au "Mungu mwenye nguvu ... Mungu anayeshambulia" tumia jina sahihi la Mungu wa Israeli.

Ni nani atatulinda dhidi ya nguvu za Mungu mwenye uwezo?

Swali hili linaonesha hisia za uoga. "Hakuna mtu atakayetulinda na Mungu huyu mwenye uwezo."

Kuweni wanaume

"kuweni na nguvu na mpigane"

1 Samuel 4:10

Israeli wakashindwa

"Waliwashinda Waisraeli" Hapa Israeli inamaanisha jeshi la Israeli.

Sanduku la Mungu lilichukuliwa

"Wafilisti walilichukua sanduku la Mungu.

1 Samuel 4:12

mavazi yamechanika na matope kichwani mwake

Hii ni njia ya kuonesha maombolezo makubwa katika desturi ya Israeli.

moyo wake ulitetemeka kwa ajili

Eli aliogopa kuwa jambo fulani baya limetokea.

Mji mzima

"Watu wote wa mji."

1 Samuel 4:14

Mtu

"Mtu wa Benyamini"

1 Samuel 4:16

Akamwambia

"Eli akasema"

Mwanangu

Eli hakuwa baba yake na Samweli. Eli anazungumza kama vile yeye ndiye baba yake na Samweli kuonesha kuwa hajamkasirikia lakini Samweli anapaswa kumsikiliza.

Israeli wamewakimbia Wafilisti

Hii inaelezea juu ya kilichotokea.

Pia kumekuwa ... watu. Pia watoto wako wawili

"Sasa nitakwambia kitu kibaya ... sasa nitakwambia kitu kibaya" au "Sio hayo tuu yaliyotokea huko ... lakini watoto wako wawili"

Sanduku la Bwana limechukuliwa

"Wafilisti wamechukua sanduku la Bwana"

1 Samuel 4:18

Alipotamka

"Yule mtu wa Benyamini alipotamka"

Kutamka

"Kuzungumza"

Shingo yake ilivunjika

"Shingo yake ilivunjika kwa sababu alianguka"

1 Samuel 4:19

Mkwe wake

"mkwe wa Eli"

Sanduku la Bwana limekamatwa

"Wafilisti wamelikamata sanduku la Bwana"

Aliyaweka moyoni yale aliyoambiwa

"aliyazingatia yale aliyoambiwa"

1 Samuel 4:21

Ikabodi

Jina hili lina maana ya "hakuna utukufu"

Kwa sababu sanduku la Mungu limetekwa nyara ... sababu sanduku la Mungu limetekwa nyala.

"Kwa sababu Wafilisti wameteka nyara sanduku la Mungu ... Kwa sababu Wafilisti wameteka nyara sanduku la Mungu"

1 Samuel 5

1 Samuel 5:1

Basi

Neno hili linaonesha mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

Nyumba ya Dagoni

Hili ni hekalu la Dagoni mungu wa Wafilisti.

Tazama Dagoni

"Walipatwa na mshangao walipoona Dagoni"

Dagoni ilianguka chini kifudifudi

Msomaji anatakiwa atambue kuwa Bwana alisababisha sanamu ianguke chini wakati wa usiku.

1 Samuel 5:4

Dagoni alikuwa ameanguka

Msomaji anatakiwa atambue kuwa Bwana alisababisha Dagoni aanguke.

Kichwa cha Dagoni na vitanga vyake viwili vilikatika na kulala

Ilikuwa kama vile Bwana ni askarialiyewashinda adui zake na kuwakata kichwa na mikono.

Mikono

Vitanga vya mikono vimanaanisha mikono yote.

Na hii ndiyo sababu, hata leo

Mwandishi anatuelezea taarifa na kutenganisha na simulizi inayosimuliwa.

1 Samuel 5:6

Mkono wa Bwana ulikuwa mzito juu ya

"Bwana aliwahukumu sana"

majipu

Huu ni ugonjwa wa ngozi.

Ashdodi na wilaya zake kwa pamoja

"Watu wote wa Ashdodi na watu wa nchi inayozunguka Ashidodi"

walipotambua

"walipofahamu"

sanduku la Mungu wa Israeli

Yaweza kuwa na maana ya 1) walikuwa wakizungumza juu ya jina kamili la Mungu wa Israeli au 2) waliamini kuwa Israeli waliabudu moja kati ya miungu mingi.

1 Samuel 5:8

wafanye juu ya sanduku la Munga wa Israeli ... Sanduku la Mungu wa Israeli lihamishwe

Yaweza kuwa na maana ya 1) walikuwa wakizungumza juu ya jina kamili la Mungu wa Israeli au 2) waliamini kuwa Israeli waliabudu moja kati ya miungu mingi.

Wakalibeba sanduku la Mungu wa Israeli.

Mwandishi anatumia jina sahihi la Mungu wa Israeli.

Mkono wa Bwana ulikuwa dhidi ya

"Bwana aliadhibu"

wote wakubwa kwa wadogo

Wao wote "wadogo kwa wakubwa, masikini na tajiri"

Majipu

Huu ni ugonjwa wa ngozi.

1 Samuel 5:10

Walipiga kelele

"walipiga kelele kwa hofu"

1 Samuel 5:11

Mungu wa Israeli

Yaweza kuwa na maana ya 1) walikuwa wakizungumza juu ya jina kamili la Mungu wa Israeli au 2) waliamini kuwa Israeli waliabudu moja kati ya miungu mingi.

kulikuwa na hofu ya kutisha mjini mwote

Watu wote wa mji waliogopa kuwa watakufa"

Mkono wa Mungu ulikuwa mzito mno huko

"Mungu aliwaadhibu sana watu huko"

Watu ambao hawakufa

Hii inaonesha kuwa watu wengi walikufa.

Majipu

Huu ni ugonjwa wa ngozi

kilio cha mji kilipanda hadi mbinguni

"Watu wa mji walilia kwa sauti kubwa" Neno "mbinguni" linamaanisha miungu ya watu. "Watu wa mji wakaililia miungu yao"

1 Samuel 6

1 Samuel 6:1

Makuhani na waganga

Hawa walikuwa ni makuhani na waganga wa kipagani walimwabudu Dagoni.

wambieni jinsi ambavyo tunapaswa kulirudisha

Wafilisti walitaka kujua namna watakavyolirudisha sanduku la Bwana bila kumkasirisha zaidi.

1 Samuel 6:3

Mungu wa Israeli

Yaweza kuwa na maana ya 1) walikuwa wakizungumza juu ya jina kamili la Mungu wa Israeli au 2) waliamini kuwa Israeli waliabudu moja kati ya miungu mingi.

kwa namna yoyote ile mpelekeeni sadakaa ya hatia

Maneno "kwa namna yoyote ile" ni namna ya kuelezea jamno. "Lazima mpeleke sadaka ya hatia"

Mtapona

"hamtaumwa tena"

Ninyi

Ni wingi inayomaanisha Wafilisti wote.

kwa nini mkono wake hadi sasa haujaondoka juu yenu

"Mkono" imetumika kuwakilisha nguvu za Mungu za kuadabisha. "kwa nini hajayaondoa mateso yenu"

Majipu

Huu ni ugonjwa wa ngozi.

Panya

Hapa anaelezea panya zaidi ya mmoja.

1 Samuel 6:5

Mifano

Mifano ni kitu kinachofanana na kitu fulani.

Majipu

Ni ugonjwa wa ngozi.

Panya

Hapa anaelezea panya zaidi ya mmoja.

ambayo huiharibu

"ambayo huangamiza"

Mungu wa Israeli

Yaweza kuwa na maana ya 1) walikuwa wakizungumza juu ya jina kamili la Mungu wa Israeli au 2) waliamini kuwa Israeli waliabudu moja kati ya miungu mingi.

ataondoa mkono wake kutoka juu yenu, kutoka juu ya miungu yenu, na kutoka juu ya nchi yenu.

ataondoa mkono wake kutoka juu yenu, kutoka juu ya miungu yenu, na kutoka juu ya nchi yenu. "ataacha kuwaadhibu ninyi na miungu yenu na nchi yenu."

Kwanini mfanye mioyo yenu kwa migumu, kama vile Wamisri na Farao walifanya mioyo yao kuwa migumu?

Makuhani na waganya wanatumia swali ili kuwafanya Wafilisti wafikirie kwa makini juu ya kile kitakachowapata ikiwa watakataa kumtii Mungu.

Kuifanya mioyo yenu kuwa migumu.

"kuacha kumtii Mungu"

Je, Wamisri hawakuwaachilia watu, na wakaondoka?

Hili swali limetumika kuwakumbusha Wafilisti kuwa Wamisri waliwaruhusu Waisraeli watoke Misri ili Mungu aache kuwaadhibu Wamisri.

1 Samuel 6:7

Ng'ombe wawili wanyonyeshao

"Ng'ombe wawili wenye ndama ambao bado wananyonya"

Ndipo mlipeleke lipate kuondoka.

Ng'ombe wawili watakwenda nyumbani kwenye ndama wao.

ikiwa watakwenda ... hadi Beth Shemeshi, basi mjue kuwa ni Bwana

Sio kawaida kwa ng'ombe kuchagua kwenda Beth Shemeshi wakati ndama wamerudi kwenye nchi ya Wafilisti.

1 Samuel 6:10

Ng'ombe wawili wanyonyeshao

"Ng'ombe wawili wenye ndama ambao bado wananyonya"

Mumbo ya majipu yao

"Mfano wa majipu yao"

Majipu

Huuu ni ugonjwa wa ngozi.

Ng'ombe waliondoka moja kwa moja kuelekea Beth Shemeshi

Ng'ombe wanaonyonyesha huwarudia ndama wao lakini ng'ombe hawa walikwenda Beth Shemeshi.

Wakipiga kelele walipokuwa wakienda

Kupiga kelele ni milio waliyokuwa wanatoa ngombe sauti zao.

hawakugeuka upande wa kushoto au kulia

"Walikwenda moja kwa moja mbele"

1 Samuel 6:13

Basi

Mwandishi anatambulisha sehemu mpya ya simulizi.

watu wa Beth Shemeshi

Hawa walikuwa Waisraeli.

Waliponyanyua macho yao

Walipotizama juu

1 Samuel 6:14

Kulikuapo jiwe kubwa mahali hapo

Jiwe hili ndilo jiwe lililotumika kama madhabahu walipotoa sadaka ya ng'ombe kama dhabihu.

Walawi walilitelemsha chini sanduku la Bwana

Hii ilitokea baada ya kutayarisha kuni zilizotokana na mkokoteni na kutengeneza moto uliotumika kutolea sadaka ya ng'ombe kwa Bwana.

Walawi walilitelemsha chini sanduku

Kutokana na sheria za Musa Walawi tuu ndio walioruhusiwa kulishughulikia sanduku.

pamoja na kasha lake lililoyatunza yale maumbo ya dhahabu,

"kasha ambalo maumbo ya dhahabu ya panya na majipu yalikuwepo"

1 Samuel 6:16

Viongozi watano wa Wafilisti

"Wafalme watano wa Wafilisti"

1 Samuel 6:17

Majipu

Huu ni ugonjwa wa ngozi

Panya

Hapa ana maana ya panya zaidi ya mmoja.

miji iliyojengewa maboma

Hii ni miji iliyozungushiwa kuta ndefu ili kuwalinda watu waliopo ndani yake wasivamiwe na adui.

Lile jiwe kubwa ... likabaki kama ushuhuda

Jiwe linafananishwa kama mtu awezaye kuona. "Jiwe kubwa ... bado liko hapo na watu wanakumbuka yaliyotokea juu yake"

Yoshua Mbeth- Shemeshi

"Yoshua toka Beth- Shemeshi"

Hadi leo

Hata wakati ambao mwandishi aliandika kitabu.

1 Samuel 6:19

walichungulia ndani ya sanduku

Sanduku lilikuwa takatifu sana na hakuna mtu aliyeruhusiwa kulitizama nadani. Makuhani tuu ndio walioruhusiwa.

Aliwaua watu sabini

"Aliwaua watu 70"

Je, ni nani awezaye kusimama mbele ya BWANA, huyu Mungu mtakatifu?

Yaweza kuwa na maana ya 1) Hakuna mtu anayeweza kushindana na Bwana kwa sababu ni mtakatifu. au 2) Yatupasa kumtafuta mtu atakayemtumikia Bwana kama Kuhani, je nani kati yetu anastahili?

Atapanda kwenda kwa nani kutoka kwetu?

Hili ni swali ambalo watu wanatafuta majibu. Yaweza kuwa na maana ya 1) "Bwana atakwenda kwa nani kutoka kwetu?" au 2) "sanduku litakwenda kwa nani kutoka kwetu?"

1 Samuel 6:21

Kiriath Yearimu

Huu ulikuwa mji katika Israeli.

1 Samuel 7

1 Samuel 7:1

Kiriath Yearimu

Hili ni jina la mahali.

Abinadabu ... Eleazari

Haya ni majina ya wanaume.

Miaka ishirini

"Miaka 20"

1 Samuel 7:3

Nyumba yote ya Israeli

"Nyumba" inamaanisha watu wanaoishi ndani ya nyumba na uzao wao. "Uzao wote wa Israeli" au "watu wote wa Israeli"

Kumrudia Bwana kwa moyo wenu wote

"Kujitoa moja kwa moja kumuabudu na kumtii Bwana tuu"

1 Samuel 7:5

Israeli wote

"Watu wote wa Israeli" au "Waisraeli wote"

Kumwaga chini mbele za Bwana

Hii yaweza kuwa na maana ya 1) watu walijinyima maji kama sehemu ya kufunga au 2) walitoa maji visimaji na kuyamwaga chini kama ishara ya kuonesha namna gani wanajutia dhambi zao.

1 Samuel 7:7

viongozi wa Wafilisti waliwashambulia Israeli

"Viongozi wa Israeli waliongoza majeshi yao kuishambulia Israeli"

atuokoe kutoka mkono wa Wafilisti

"atuokoe toka kwenye jeshi la Wafilisti"

1 Samuel 7:9

ndama mchanga

Ndama ambaye bado ananyonya maziwa ya mama yake.

Akamlilia

Akaomba msaada

Bwana akamjibu

Bwana akafanya yale ambayo Samweli alimuomba ayafanye.

1 Samuel 7:10

Hata Samweli ... Beth kari

Hii inaelezea kuwa mwandishi anamaanisha kuwa "Bwana alimjibu"

Kuwachanganya

Kusababisha Wafilisti washindwe kufikiri vizuri na wasijue la kufanya.

Wakashindwa mbele ya Israeli

Hii inaweza kutafsiriwa kama 1) Bwana akawafanya washindwe mbele ya Israeli" au "Israeli wakawashinda wao."

Kuwashindwa

Kuwashinda watu ni kuwadhibiti kabla hawasababisha maafa.

Beth kari

Hili ni jina la mji.

1 Samuel 7:12

Akachukua jiwe na kulisimamisha

Waisraeli na watu wengine wa nchi ile waliweka jiwe kubwa mahali ambapo matukio ya muhimu yalitokea kama kumbukumbu ya msaada wa Mungu.

Mispa ... Sheni

Haya ni majina ya mahali.

1 Samuel 7:13

Kwa hiyo, Wafilisti walishindwa

Mwandishi anamaliza kuwa kutuelezea namna ambavyo Wafilisti walishindwa.

Wafilisti walishindwa

Bwana aliwafanya Wafilisti washindwe.

hawakuingia katika mipaka ya Israeli

Wafilisti hawakuingia katika mpaka wa Israeli ili kuwashambulia.

Mkono wa Bwana ulikuwa dhidi ya Wafilisti.

"Bwana alitumia nguvu zake dhidi ya Wafilisti"

Miji ... kutoka kwa Israeli ikarudishwa kwa Israeli

Hii inaweza kuwa na maana ya 1) "Bwana aliirudisha miji ya nchi ya Israeli ... toka Israeli" au 2) "watu wa Israeli waliweza kuidai miji yao ... toka Israeli"

1 Samuel 7:15

Wakazunguka

Wakasafiri toka sehemu moja mpaka nyingine kwa kuzunguka.

Aliamua migogoro

Migogoro ni malumbano au kutokuelewana kati ya watu wawili au zaidi.

1 Samuel 8

1 Samuel 8:1

walipiga mbio kutafuta mapato ya udhalimu

"Walifanya kazi kwa nguvu ili kupata mapato kwa njia ya udhalimu"

Kupotosha hukumu

"Kutoa hukumu kwa kuwapendelea wanaofanya uovu"

1 Samuel 8:4

hawaenendi katika njia zako

"hawafanyi vitu unavyofanya" au "hawafanyi kama vile unavyofanya wewe"

Tuchagulie mfalme wakutuamua kama yalivyo mataifa yote

Hii yaweza kuwa na maana ya 1) "Tuchagulie mfalme kama wafalme wa mataifa yote ili atuamue" au Tuchagulie mfalme atakayetuamua kama wafalme wa mataifa wanavyowaamua wao"

Tuchagulie mfalme wakutuamua

Viongozi waliamini vibaya kuwa mfalme na wana wake wataongoza kwa haki.

1 Samuel 8:6

Lakini haikumpendeza Sameli ... Utupatie mfalme

Samweli hakuwa na furaha kwamba watu hawakutaka yeye awaondoe watoto wake waliokuwa waovu na kumteua mwamuzi mwingine lakini walitaka mfalme wa kutawala juu yao kama nchi nyingine zinavyofanya.

Sikiliza sauti ya watu

Hapa neno "sauti" linamaana ya mapenzi au matakwa ya watu. "Fanya kama vile watu wanavyotaka"

bali wamenikataa mimi

Bwana alijua kuwa watu hawakuwakataa viongozi waovu tuu bali walimkataa yeye kama mfalme wao.

1 Samuel 8:8

Niliwatoa Misrai

Hiki ni kitendo cha Bwana kuwatoa Waisraeli utumwani Misri miaka mingi iliyopita.

Sasa wasikilize

"Sasa fanya kama vile wanavyokuomba ufanye"

Waonye sawasawa

"uwe makini unapowaonya"

1 Samuel 8:10

Hivi ndivyo mfalme atakavyotawala ... atachukua

Matendo ya mfalme yatakuwa kuchukua. Huu ni mwanzo wa vitu ambavyo mfalme atachukua.

Hivi ndivyo jinsi mfalme atakavyowatawala.

"Hivi ndivyo mfalme atakayetawala juu yenu atakavyofanya"

Atawaweka juu ya magari yake

"Atawafanya waendeshe magari vitani"

Kuwa wapanda farasi wake

Wataendesha farasi kwenda vitani.

1 Samuel 8:13

Taarifa ya jumla:

Samweli anaendelea kuwaambia vitu ambavyo mfalme atavichukua.

kuwa watengeneza manukato

"Kutengeneza mafuta yanayonukia vizuri kwa ajili ya kujipaka mwilini"

mizeituni

"mashamba ya miti ya mizeituni"

moja ya kumi ya nafaka zenu

Watagawanya nafaka zao katika mafungu kumi yaliyosawa kisha kutoa fungu moja maafisa wa mfalme na watumishi.

moja ya kumi ya mizabibu

Watagawanya divai waliyoipata toka kwenye mizabibu katika mafungu kumi kisha kutoa fungu moja kwa maafisa wa mfalme na watumishi.

Afisa

Ni kiongozi katika jeshi la mfalme.

1 Samuel 8:16

Taarifa ya jumla:

Samweli anaendelea kuwaambia vitu ambavyo mfalme atavichukua.

moja ya kumi ya mifugo yenu

Watagawanya mifugo yao katika mafungu kumi yaliyosawa kisha kutoa fungu moja maafisa wa mfalme na watumishi.

mtakuwa watumwa wake

"mtahisi kama vile nyie ni watumwa wake"

Mtalia

Yaweza kuwa na maana ya 1)watu watamuomba Bwana awaokoe toka kwa mfalme au 2) watu watamuomba mfalme aache kuwanyanyasa.

1 Samuel 8:21

akayarudia katika masiko ya Bwana.

"Masikio ya Bwana" inamuelezea Bwana. Samweli alimuomba Bwana kwa kurudia yote ambayo watu walimwambia.

Sikiliza sauti yao

"Wasikilize watu"

uwafanyie mfalme

"Mfanye mtu kuwa mfalme juu yao"

arudi mjini kwake

"akarudi nyumbani"

1 Samuel 9

1 Samuel 9:1

Taarifa ya jumla

Mwandishi anatupa taarifa ya jumla katika mistari hii.

mtu mashuhuri

Mtu ambaye watu wanamuheshimu na wanasikiliza anachokisema.

Kishi ... Abieli ... Zerori ... Bekorathi ... Afia

Haya ni majina ya wanaume katika ukoo ya familia ya sauli.

Mbenyamini

Mbenyamini ni mtu anayetoka katika kabila la Wabenyamini.

mzuri wa uso

Mtu mwenye muonekano mzuri.

Kutoka mabegani kwenda juu alikuwa mrefu kuliko watu wengine

Watu wengine warefu katika Israeli hawakumfikia mabegani wake.

1 Samuel 9:3

Sasa

Mwandishi ameanza sehemu mpya ya simulizi.

amka

"acha kufanya unachokifanya"

nchi ya vilima vilima ya Efraimu ... nchi ya Shalisha ... nchi ya Shaalimu ... nchi ya Wabenyamini

Haya ni maeneo katika Israeli.

hawakuwaona ... hawakuwa huko ... hawakuwaona

Hapa wanazungumziwa punda.

1 Samuel 9:5

nchi ya Sufu

Hili ni eneo katika Israeli kaskazini mwa Yerusalemu.

Mtu wa Mungu

Mara nyingi humaanisha nabii wa Bwana. "Mtu anayesikia na kusema maneno toka kwa Mungu"

tupitie wapi katika safari yetu

"tupite njia gani ili tuwapate punda wetu"

1 Samuel 9:7

twaweza kumpelekea nini?

Kupeleka zawadi ni alama ya heshima kwa mtu wa Mungu.

Mtu wa Mungu

Mara nyingi humaanisha nabii wa Bwana. "Mtu anayesikia na kusema maneno toka kwa Mungu"

robo ya shekeli

Robo ya shekeli ni aina ya fedha ambayo ilitumika katika agano la kale.

1 Samuel 9:9

Zamani katika Israeli ... mwonaji

Hii ni taarifa ya desturi ambayo iliongezwa na mwandishi wa Kiebrania.

Kwa maana nabii wa leo, zamani aliitwa Mwonaji

"Mwonaji ni jina la zamani la nabii"

1 Samuel 9:12

leo watu wanatoa dhabihu

Hizi ni kama sikukuu au dhabihu za matunda ya kwanza, sio dhabihu za dhambi ambazo lazima zifanyikie katika hema.

1 Samuel 9:14

akipanda kwenda mahali pa juu

Hapa ni mahali ambapo watu wamepafanya kuwa mahali patakatifu pa kutolea dhabihu na sadaka kwa Bwana.

1 Samuel 9:15

Taarifa ya jumla:

Mwandishi ameacha kutuelezea simulizi na anatoa taarifa ya jumla ili msomaji aelewe ni kitu gani kinafuata.

nawe utamtia mafuta awe mkuu

Neno mkuu limetumika badala ya neno mfalme. Huyu ni mtu ambaye Bwana amemchagua awe mfalme wa Israeli.

nchi ya Benyamini

"nchi ambayo watu wa kabila la Benyamini waliishi"

kutoka kwenye mkono wa Wafilisti

"Ktutoka kwenye utawala wa Wafilisti"

Kwa kuwa nimewaonea huruma watu wangu

"Watu wangu wanateseka na ninataka kuwasaidia"

1 Samuel 9:17

Bwana akamwambia

"Bwana akamwambia Samweli"

Mwonaji

"Nabii wa Bwana"

1 Samuel 9:20

Na yote yaliyotamanika kwa ajili ya Israeli yanamwangukia nani? Siyo kwako na nyumba ya baba yako yote?

Maswali haya yanaelezea kwa undani kuthibitisha kuwa Sauli ndiye aliyechaguliwa na Bwana kuwa Mfalme wa Israeli.

Siyo mimi Mbenyamini ... ya Israeli? Kwa nini basi unaniambia kwa namna hii?

Sauli anashangaa kwa sababu Waisraeli wwengine walilichukulia kabila la Benyamini kama kabila ovu na Wabenyamini walichukulia ukoo aliotoka Sauli kuwa haukuwa wa muhimu.

1 Samuel 9:22

Ukumbini

Mwandishi anaonesha kuwa karibu na sehemu ya kutolea dhabihu kulikuwa na jengo kubwa ambalo watu walikuwa wakila pamoja huko.

mahali pa heshima

"Hiki ni kiti cha heshima"

thelathini

"30"

1 Samuel 9:23

paja lililokuwa limeinuliwa katika dhabihu

Kuhani aliyeinua paja katika dhabuhu ndiye anayepaswa kula. Samweli alimfanya Sauli ale ili kuonesha kuwa kuwa mfalme ni kazi takatifu.

Kilichokuwa pamoja nayo

Yaweza kuwa na maana ya 1)chakula kingine ambacho Sauli alikula pamoja na nyama au 2) sehemu nyingine ya ng'ombe.

Kisha Samweli akasema

Hii yaweza kuwa na maana ya "Mpishi akasema."

Na kwa sasa waweza kusema, 'Nimewaalika watu.'

Yaweza kuwa na maana ya 1) Sauli anaweza kusema kuwa aliwaalika watu au 2) Samweli aliwaalika watu

1 Samuel 9:25

darini

Hii ilikuwa sehemu ya kawaida kwa familia na wageni kula na kulala. Huwa na ubaridi jioni usiku kuliko sehemu nyingine za nyumba.

Samweli alimwita Sauli darini na kusema

"Sauli alipokuwa amelala darini Samweli alimuita na kusema"

1 Samuel 9:27

mbele yetu ... na alitangulia mbele ... Lakini wewe sharti usubiri

Yaweza kuwa na maana ya "mbele yetu na atakapokwenda mbele yetu yakupasa usubiri"

nipate kukuambia ujumbe wa Mungu

"Ili nikuambie ujumbe wa Mungu kwa ajili yako"

1 Samuel 10

1 Samuel 10:1

akachukua chupa ya mafuta, akayamimina juu ya kichwa cha Sauli

Katika tamaduni za Israeli nabii inapomimina mafuta katika kichwa cha mtu huyo mtu anapokea baraka toka kwa Bwana.

Chupa

Ni chombo kidogo kilichotengenezwa kwa udongo.

Je, Mungu hajakutia mafuta uwe mtawala juu ya urithi wake?

Samweli anajua jibu la swali hili. Anamkumbusha Sauli kuwa Bwana amemchagua yeye kuwa mfalme wa Israeli.

Selsa

Hili ni jina la mahali.

Nitafanya nini kuhusu mwanangu?

Baba yake na Sauli anaanza kuwa na hofu juu ya mtoto wake na anataka kumtafuta.

1 Samuel 10:3

Tabori

Hili ni jina la mahali.

kuchukua toka mikononi mwao

"kuchukua toka kwao" au "kukubali"

1 Samuel 10:5

Matari

Ni kifaa cha muziki kama ngoma ambacho kinaweza kupigwa na chenye vipande vya chupa huzunguka kifaa hicho, vipande hivi hulia kifaa kinapotikiswa.

Roho wa Bwana atakujaza

Hii inamaana kuwa roho wa Bwana atamchochea Sauli. Atamfanya Sauli atoe unabii na kuwa tofauti na watu wengine.

1 Samuel 10:7

fanya lolote ambalo mikono yako itaona ifanye

Hapa Samweli anazungumza juu ya mikono ya Sauli. "fanya kile ambacho unafikiri ni sahihi kufanya"

1 Samuel 10:9

Mungu akampa moyo mwingine

Mungu akamfanya Samweli afikiri tofauti na alivyofikiri mwanzo.

Roho ya Mungu ikamjilia

"Roho ya Mungu ikamtawala kabisa.

1 Samuel 10:11

Kitu gani kimempata mtoto wa Kishi?

Hii inaweza kuwa na maana ya 1) watu wanauliza ili kupata taarifa au 2) yaweza kuwa Swali linaloonesha kuwa Sauli sio wa muhimu. "Kishi sio mtu wa muhimu hivyo haiwezekani mtoto wake akawa nabii"

Mwana wa Kishi

"Sauli, mwana wa Kishi"

Na ni nani baba yao?

Swali hili linawakumbusha watu kuwa kuwa nabii haina uhusiano na baba yako ni nani. "Haijalishi Manabii hawa wazazi wao ni akina nani"

Kwa sababu ya jambo hili, ukawapo msemo, "Hivi Sauli naye ni mmoja wa manabii?"

"Na hii ndiyo sababu, wakati ambapo watu hawakuamini baadhi ya taarifa walifikiri juu ya kilichotokea kwa Sauli na kusema 'Hivi Sauli naye ni mmoja wa manabii?'"

Hivi Sauli naye ni mmoja wa manabii?

Kwa Sababu Sauli ni mmoja wa manabii watu walifikiri kuwa hata watu wasiokuwa na umuhimu wanaweza kuwa manabii.

1 Samuel 10:14

Ndipo baba yake mdogo na Sauli akamwambia

"Ndipo kaka yake na baba yake na Sauli akamwambia Sauli"

Hakumwambia kuhusu swala la ufalme

"Sauli hakumwambia baba yake mdogo kuwa Mungu amemchagua kuwa mfalme wa Israeli"

1 Samuel 10:17

Niliwatoa Israeli kutoka Misri

"Niliwatoa watu wa Israeli kutoka Misri"

Leo

"sasa"

Mkono wa Wamisri ... mkono wa falme zote

"Mkono" inamaanisha mguvu. "Nguvu za Wamisri ... nguvu za mataifa yote"

Tuwekee mfalme juu yetu

Tupe mfalme wa kutuongoza.

jihudhurisheni wenyewe mbele za BWANA kwa kabila na jamaa zenu

"Wakusanye makabila na jamaa na msimame mbele za Bwana"

1 Samuel 10:20

Kabila la Benyamini lilichaguliwa ... jamaa ya Wamatri ikachaguliwa ... Sauli mwana wa Kishi akachaguliwa

"Bwana alichagua kabila la Benyamini... Bwana alichagua jamaa ya Wamatri... Bwana alimchagua Sauli mwana wa Kishi"

1 Samuel 10:22

alikuwa mrefu kuliko watu wote kuanzia mabega yake kwenda juu

Watu wengine warefu katika Israeli hawakumfikia mabegani wake.

1 Samuel 10:25

desturi na sheria za ufalme

"Mambo ambayo mfalme atawalazimisha wayafanye na mambo yote ambayo mfalme anapaswa kuyafanya"

1 Samuel 10:26

wenye mioyo iliyoguswa na Mungu

Mungu anapougusa mioyo ya watu ina maana ya kuwa Mungu ameweka kitu kwenye mioyo yao na kuwafanya watende jambo fulani.

Huyu mtu atatuokoaje?

"mtu huyu hana nguvu za kutuokoa"

Walimdharau

"Hawakumpenda"

1 Samuel 11

1 Samuel 11:1

Nahashi

Alikwa Mwamoni, uzao wa Lutu.

Yabeshi Gileadi

Hili ni jina la mahali.

Niling'oa

"Nilikata"

Kuleta fedheha

"kuleta aibu"

1 Samuel 11:3

Siku saba

"Siku 7"

1 Samuel 11:4

Gibea

Hili ni jina la mahali.

1 Samuel 11:6

Roho ya Mungu ikamjia kwa nguvu

Roho ya Bwana ikamchochea Sauli. Ikamfanya Sauli asababishe watu wamuogope kwa kumuheshimu kama mfalme wao na kujiunga na jeshi lake.

asiyejitokeza akimfuata

Sauli aliwaita watu wote wa Israeli waende kupigana dhidi ya Nahashi na Waamoni.

Na hofu ya Bwana ikawaingia watu

Bwana akasababisha watu wamuogope na kumuheshimu Sauli kama mfalme wao.

Beseki

Hili ni jina la mji ulikokuwa karibu na Yabeshi Gileadi.

watu wa Israeli walikuwa mia tatu elfu, na watu wa Yuda elfu thelathini.

"Watu wa Israeli walikuwa 300,000 na watu wa yuda walikuwa 30,000"

1 Samuel 11:9

Wakawaambia wale wajumbe

Hapa anazungumziwa Samweli na Sauli.

wakati wa jua kali

"kabla ya mchana"

Yabeshi Gileadi ... Yabeshi

Haya ni majina ya mahali.

Nahashi

Hili ni jina la mfalme.

1 Samuel 11:11

wakati wa asubuhi

Mda huu ni kabla ya mapambazuko ambapo watu wengi kwenye kambi walikuwa bado wamelala.

1 Samuel 11:14

Wakamsimika Sauli kuwa mfalme mbele za Bwana

"Wakamsimika Sauli kuwa mfalme wakati Bwana anaangalia"

Na huko walitoa sadaka za amani mbele za Bwana

Sehemu ya huduma ya Samweli kwa Bwana ni kutoa dhabihu japokuwa hakutoka katika ukoo wa Haruni wala wa Lawi.

1 Samuel 12

1 Samuel 12:1

yupo hapa mfalme aliyeko mbele yenu ... nami nimekuwako mbele yenu

Sentensi hizi zinaonesha kuwa watu waliweza kuona maisha ambayo Sauli na Samweli waliishi. "Maisha ya mfalme yalionekana ... maisha yangu yalionekana"

1 Samuel 12:3

Mimi niko hapa , Nishuhudieni mbele za BWANA na mbele za mtiwa mafuta wake.

Samweli anawasihi watu waeleze ikiwa amefanya jambo lolote baya.

Nimechukua ng'ombe wa nani? Nimechukua punda wa nani?

Samweli anatumia maswali kuwakumbusha watu kuwa hakuwahi kuwaibia wanyama wao.

Ni nani nimemdhulumu?

Samweli anatumia swali hili kuonesha kuwa amekuwa mkweli wakati wote.

Nishuhudieni, nami nitawarudishia

"Ikiwa nimefanya mabaya yoyote semeni sasa na nitawalipa mnavyonidai."

1 Samuel 12:4

kutoka mkono wa mtu yeyote ... kwenye mkono wangu

Hii ni namna nzuri ya kusema kuwa hakuiba waka kutoa au kupokea rushwa.

1 Samuel 12:6

matendo yote ya haki ya BWANA

Samweli anawaonesha historia ya Bwana alivyokuwa anawatendea Waisraeli, namna ilivyojawa na mambo mema na kusudi.

1 Samuel 12:8

Yakobo ... Musa ... Haruni ... Sisera

Haya ni majina ya watu.

Hazori

Hili ni jina la mahali.

akawauza

Hii inaelezea namna ambavyo Mungu aliwatoa juu ya adui zao kama watumwa.

Kwenye mikono ya Sisera ... Wafilisti ... Mfalme wa Moabu

"kwenye nguvu za Sisera ... Wafilisti na mfalme wa Moabu"

1 Samuel 12:10

Wakamlilia Bwana

Hawa ni taifa la Israeli.

tumewatumikia Mabaali na Mashtorethi

Kumtumikia imetumika hapa kama kumwabudu, "waliabudu miungu ya uongo"

Mkono wa adui zako

"Nguvu au utawala wa adui zako"

Yerubu Baali

Hili ni jina la heshima na nguvu ya kupigana na Mungu wauongo.

Bwana akawatuma ... na akawapa ushindi

Samweli anasimulia simulizi ya namna ambavyo Mungu alifanya baada ya watu kutubu dhambi zao na kuomba msaada.

Yerubu Baali, Bedani, Yefta na Samweli

Haya ni majina ya baadhi ya waamuzi ambao Mungu aliwainua.

1 Samuel 12:12

'Hapana! Badala yake, mfalme awepo atawale juu yetu

Sentensi hii inaonesha namna ambavyo taifa la Israeli lilimpinga Samweli alipowaambia kuwa wamwamini Mungu kwa sababu Mungu aliwaokoa zamani.

ambaye mmemchagua, ambaye mlimuomba

Sentensi hizi zina maana moja na zinasisitiza kuwa huyu ndiye mfalme ambaye watu wanamtaka.

1 Samuel 12:14

mnamuhofu ... mtumikieni ... mtiini.... msimuasi

Maneno haya yanayofanana yametumika ili kusisitiza umuhimu wa jambo hili.

dipo mkono wa BWANA utakuwa juu yenu, kama ulivyokuwa juu ya babu zenu.

"Bwana atawaadhibu ninyi kama walivyowaadhibu babu zenu"

1 Samuel 12:16

Mbele ya macho yenu

"macho" inawakilisha watu wa taifa la Israeli.

Je, leo si mavuno ya ngano?

Samweli anajua kuwa ni wakati wa mavuno. "Ni wakati wa mavuno na mvua hainyeshi katika wakati huu"

Akatuma radi na mvua

Samweli anamuomba Bwana awaadhibu Israeli kwa kutaka mfalme kwa mumuomba atume mvua ya radi wakati wa mavuno ambayo itaharibu mavuno.

1 Samuel 12:19

Ili tusife

Adhabu ya dhambi ni kifo. Taifa la Israeli liliona Bwana akiharibu mataifa yaliyowanyanyasa. Walikuwa na wasiwasi kuwa wataharibiwa kama mataifa mengine.

Msiogope

Watu walifanya maovu na waliogopa kuwa Mungu atawaharibu. "Msiogope kuwa Mungu atakasirika na kuwaharibu kwa sababu ya dhambi hii"

msigeuke na kufuata mambo matupu

"msikimbilie kuabudu miungu ya uongo"

1 Samuel 12:22

Kwa ajili ya jina lake kuu

"Hivyo watu wataendelea kumuheshimu na kumtii Bwana"

Kwangu mimi, iwe mbali nami kumtenda BWANA dhambi kwa kuacha kuwaombea ninyi.

Watu walishikwa na hofu kwa sababu ya radi na mvua ambavyo Bwana alivituma Samweli alipoomba. Watu wengine walihisi kuwa Samweli atatumia maombi yake kuwaangamiza.

1 Samuel 13

1 Samuel 13:1

Taarifa ya jumla:

Samweli anawakumbusha watu kumfuata Bwana.

Sauli alikwa na umri wa miaka thelathini ... juu ya Israeli

Maneno katika mistari hii yamenukuliwa toka katika vitabu vya zamani hivyo kwa matoleo ya kisasa kunaweza kuwa na tafsiri ya tofauti.

Askari waliobaki aliwarudisha nyumbani

"Aliwarudisha askari waliobaki nyumbani"

Aliwachagua watu elfu tatu

"Aliwachagua watu 3,000"

Elfu mbili walikuwa pamoja naye huko Mikmashi

"2,000 walikuwa pamoja naye huko Mikmashi"

Gibea ya Benyamini

Gibea ni jina la mji.

1 Samuel 13:3

ngome ya Wafilisti

"ngome ya jeshi la Wafilisti" au "kambi ya jeshi la Wafilisti"

Geba

Hili ni jina la mji ambapo ngome ya Wafilisti ilikuwepo huko.

Israeli yote imesikia kwamba Sauli ameipiga

Hii yaweza kuwa na maana ya 1)Sauli alichukua jukumu la vitendo vya Yonathani au 2)Sauli alichukua pongezi kwa vitendo vya Yonathani.

Uvundo

Taifa la Israeli linafananishwa na uvundo.

Ndipo askari wakaitwa kwa pamoja kuungana na Sauli huko Gilgali.

"Sauli akawaita askari kwa pamoja kuungana naye huko Gilgali"

1 Samuel 13:5

elfu tatu ... elfu sita

"3,000 ... 6,000"

majeshi mengi kama mchanga ufukoni mwa bahari

Kundi la askari walikuwa wengi na ilikuwa ngumu kuwahesabu.

Mikimashi

Hili ni jina la mahali.

Beth aveni.

Hili ni jina la mahali.

1 Samuel 13:6

Taarifa ya jumla:

Wafilisti walikusanyika ili kupigana dhidi ya Israeli.

Watu

Taifa la Israeli.

watu walikata tamaa

"watu waliogopa sana"

nchi ya Gadi na Gileadi

Haya ni majina ya miji.

Walimfuata wakitetemeka

Watu walikuwa wanogopa sana.

1 Samuel 13:8

muda uliopangwa na Samweli.

"kutokana na muda ambao Samweli alimwambia kuwa atakuja"

watu wakatawanyika mbali na Sauli

"Watu wakaanza kumuacha Sauli"

Kisha akatoa sadaka ya kuteketezwa

Ukoo wa Haruni tuu ndio ulioruhusiwa kutoa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana.

1 Samuel 13:11

Umefanya nini?

Samweli alikuwa haulizi swali ila alikuwa akimkemea Sauli. Sauli akaanza kujitetea japokuwa alikosea.

Mikmashi

Hili ni jina la mahali.

1 Samuel 13:13

Taarifa ya jumla:

Sauli anamwambia Samweli kwa nini amefanya kitendo hicho kama kuhani na kutoa sadaka.

Hukuheshimu amri ya BWANA

Sauli alipaswa amsubiri Sauli afike na atoe sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana na sio kufanya hivyo yeye.

Aliutengeneza utawala wako

"Aliuweka utawala wako" au "aliuchagua utawala wako"

utawala wako hautaendelea

"Utawala wako utakoma muda si mrefu"

mtu anayekubaliwa na moyo wake

"Mtu atakayefuata amri zake"

1 Samuel 13:15

Samweli akasimama na kwenda

"Samweli akaondoka na kwenda mpaka"

mpaka Gilgali

Gilgali ni jina la mji.

Gibea ya Benyamini

Gibea ni jina la mji.

Watu mia sita

"600"

Geba ya Benyamimni

Geba ni mji.

Wafilisti wakapiga kambi huko Mikmashi

Mikmashi ni jina la mahali.

1 Samuel 13:17

Wateka nyara

Wateka nyara ni askari jeshi wanovamia vijiji vya adui zao kwa ajili ya chakula na mahitaji mengine.

Ofra, hadi nchi ya Shuali ... Bethholoni ...bonde la Seboimu

Haya ni majina ya mahali.

1 Samuel 13:19

Taarifa ya jumla:

Msimuliajia nasimulia kusuhu wafua vyuma wa Israeli.

Hakuna hata mhunzi aliyeonekana

"Hakuna mtu atakayempata mhunzi"

Mhuzni

Mhuzi ni mtu anayetengeneza vifaa vya chuma na silaha.

kunoa jembe lake

Jembe ni kifaa cha chuma ambacho hutumika kulimia ardhini kwa ajili ya kupanda mazao.

sululu ... shoka ... mundu

Hivi ni vifaa vya kwenye bustani

Sululu

Ni kifaa chenye ncha kali kinachotumika kupasulia udongo mgumu.

mundu

Ni kifaa cha ncha kali kinachotumika kukatia majani na nafaka.

Theluthi mbili ya shekeli

Shekeli imegawanywa katika sehemu tatu na mbili ya tau imetolewa.

kunyoosha michokoo

Kuondoa mchokoo na kumfanya ng'ombe anyooke ili aweze kutumika.

1 Samuel 13:22

Taarifa ya jumla

Simulizi inaendelea:

hakukuwa na mapanga au mikuki

Hii inaelezea ni kwa nini jeshi la Sauli lilikuwa linaogopa. Hawakuwa na silaha kwa ajili ya mapigano.

1 Samuel 14

1 Samuel 14:1

Taarifa ya jumla:

Yonathani anaanza uvamizi wake wa pili katika jeshi la Wafilisti.

mbeba silaha wake aliye mdogo,

Kijana mdogo aliyekuwa na jukumu la kubeba silaha za bwana wake kwa ajili ya vita.

gome ya Wafilisti

Hii ni sehemu ambayo jeshi la Wafilisti iliweka kambi.

1 Samuel 14:2

Gibea

Hili ni jina la kilima kaskazini mwa Yerusalemu.

chini ya mti wa mkomamanga

Ni mti ambao matunda yake yana ganda gumu, la duara jekundu na lenye mbegu nyingi kwa ajili ya kula.

ulio katika Migroni

Migroni ni eneo lililopo Kaskazini mwa Yerusalemu.

watu mia sita walikuwa pamoja naye

"watu 600 walikuwa pamoja naye"

mwana wa Ahitubu (nduguye Ikabodi)

"Ahitubu" n"a Ikabodi" ni majina ya wanaume.

Finehasi mwana wa Eli

Finehasi alikwa mmoja wa makuhani.

1 Samuel 14:4

Jabali moja liliitwa Bosesi

Jabali ni mwamba wenye mteremko mkali. Jabali hili lilijulikana sana na lilipewa jina la "Bosesi"

Jabali lingine liliitwa Sene

Hili lilikuwa jina la jabali lingine.

Mikmashi

"Mikmashi" ulikuwa mji kaskazini mwaYerusalemu.

Geba

"Geba" ulikuwa mji kaskazini mwaYerusalemu.

1 Samuel 14:6

kijana mbeba silaha wake

Kijana mdogo aliyekuwa na jukumu la kubeba silaha za bwana wake kwa ajili ya vita.

wasiotahiriwa

Hili ni neno lililotumika kuwaelezea watu ambao hawakuwa Wayahudi.

atatenda kwa niaba yetu

"atatusaidia"

hakuna kitu kiwezacho kumzuia Bwana asiokoe

"Bwana anaweza kuokoa"

kwa wengi au kwa watu wachache

"Kwa idadi yoyote ya watu"

kila kitu kilicho ndani ya moyo wako

"kila kitu unachotamani kufanya"

1 Samuel 14:8

hatutavuka kwenda kwao

"hatutakwenda katika upande mwingine wa bonde ambapo Wafilisti wapo"

amewaweka mkononi mwetu

"atatuwezesha kuwashinda"

Hii ndiyo itakuwa ishara yetu

"Hii itathibitisha kuwa Bwana atakuwa pamoja nasi"

1 Samuel 14:11

wakajifunua mbele ya ngome ya Wafilisti

"wakaruhusu askari wa Wafilisti wawaone"

mgome

"Kambi ya jeshi"

wanakuja kutokea kwenye mashimo walimojificha

Wafilisti wanaelezea kuwa Waebrania walijificha kwenye mashimo chini kama wanyama.

tutawaonesha jambo

"tutawafundisha jambo"

amewaweka katika mkono wa Israeli

"Atawawezesha Waisraeli kuwashinda"

1 Samuel 14:13

Yonathani alipanda juu kwa mikono na miguu yake

"Hivyo Yonathani akapanda juu kwa kutumia mikono na miguu yake kwa sababu kulikuwa na

Wafilisti waliuwawa mbele ya Yonathani

"Yonathani aliwaua Wafilisti"

mbeba silaha wake akiwaua baadhi nyuma yake

"Mbeba silaha wa Yonathani alimfuata na kuwaua askari wa Wafilisti"

1 Samuel 14:15

Kukawa na hofu

"kulikuwa na woga sana"

Wateka nyara

Wafilisti waliokuwa wakiteka nyara miji ya Israeli.

Nchi ikatetemeka

"Mungu alisababisha nchi ikatetemeka"

1 Samuel 14:16

Gibea

Hili ni jina la mji.

likitawanyika ... wakienda kule na huku

Maneno haya yanamaana sawa yakisisitiza kuwa askari walikuwa wakikimbia kila mahali.

1 Samuel 14:18

Lete hapa Sanduku la Mungu

Matoleo mapya yameandika "naivera" badala ya "sanduku la Mungu"

ghasia

"kelele nyingi na kuchanganyikiwa"

Acha kazi unayofanya

"Acha kufanya jambo unalofanya" Sauli hakutaka Ahiya aendelee kulitumia sanduku la Mungu kuulizia uelekeo"

1 Samuel 14:20

watu aliokuwa nao

Jeshi la Israeli ambalo lilibaki pamoja na Sauli.

Upanga wa kila Mfilisti ulikuwa juu ya Mfilisti mwenzake

"Wafilisti walipigana wao kwa wao kwa upanga"

1 Samuel 14:22

Waisraeli wote waliokuwa wamejificha katika milima

Askari hawa walijificha kwa sababu waliwaogopa Wafilisti.

Beth aveni

Hili ni jina la sehemu katika Israeli.

1 Samuel 14:24

Hivyo hakuna hata mmoja kati ya watu wote aliyeonja chakula

Ilieleweka kwa watu kuwa chini ya kiapo cha Sauli hakuna chakula kilichoruhusiwa.

Watu wakaingia msituni

Askari wa Wafilisti walikimbilia msituni na askari wa Israeli wakawafuata.

Asali ilitiririka

Hii inasisitiza kuwa "kulikuwa na asali nyingi kila mahali"

hakuna aliyeweka mkono wake kinywani

"hakuna aliyekula chochote"

watu waliogopa kiapo

Watu hawakukiogopa kiapo ila waliogopa adhabu iliyoambatana na kuvunja kiapo.

1 Samuel 14:27

Taarifa ya jumla:

Yonathani anagundua juu ya kiapo cha baba yake.

amewaagiza watu kwa kiapo

"aliwaamuru watu kwa kutii kiapo"

akanyoosha mkono wake hadi kinywani mwake

"Alikula asali"

macho yake yakaangaziwa

Sentensi hii inamaanisha kuwa alipata nguvu. "alirejeshewa nguvu zake"

1 Samuel 14:29

nchi

Hii inawakilisha taifa la Israeli.

Macho yangu yalitiwa nuru

Sentensi hii inamaanisha kuwa alipata nguvu. "alirejeshewa nguvu zake"

Je, siyo vizuri sana kama watu ... walizopata?

Yonathani anatumia swali hili kueleza kuwa watu walitakiwa waruhusiwe kula. "Ushindi wetu ungekuwa mzuri sana ikiwa watu wangekuwa huru kula nyara walizochukua toka kwa adui zao"

Nyara

Hivi ni vitu ambavyo watu huchukua wakiwa vitani toka kwa adui zao.

Kwa sababu sasa mauaji hayakuwa makubwa

Kwa sababu askari hawakuweza kula wakati wa vita walikuwa dhaifu. Kwa sababu hii hawakuweza kuwaua Wafilisti wengi.

1 Samuel 14:31

Taarifa ya jumla:

Maneno ya Yonathani yakawafanya watu wamtende Mungu dhambi katika njaa yao kuu.

Mikmashi

Hili ni jina la mji.

Aiyaloni

"Aiyaloni" ni sehemu huko Zebuloni Israeli.

Watu

Hawa ni Waisraeli.

walikula nyama zao pamoja na damu.

Walikuwa na njaa sana hivyo walikula mpaka damu. Hapa walikiuka sharia aliyopewa Munsa kwa ajili ya taifa la Israeli.

1 Samuel 14:33

kula pamoja na damu

Hii ilikuwa ukiukwaji wa sharia ambayo Musa alipewa kwa ajili ya taifa la Israeli.

Mmetenda isivyo haki

Sauli analishitaki jeshi lake lote kwa kutenda bila uaminifu japokuwa sio wote waliofanya hivyo.

Sasa, viringisheni jiwe kubwa kwangu

Jiwe lingewashikilia wanyama na kusababisha damu ikauke haraka kwenye miili yao.

wawachinje hapa, na kuwala

Hii ingemuwezesha Sauli kuona kuwa damu ilikauka toka kwa wanyama.

1 Samuel 14:35

Taarifa ya jumla:

Sauli anawaambia watu wawawekee wanyama jiwe kubwa ili kuwaua na kuwala.

Sauli akamjengea Bwana madhabahu

Haipo wazi kama Sauli alijenga madhabahu hii kwa jiwe kubwa ambalo watu walimletea.

1 Samuel 14:36

Taarifa ya jumla:

Sauli anataka kuendelea kupigana na Wafilisti.

tusimwache hata mtu mmoja akiwa hai

"Tumuue kila mtu"

Fanya unaloona linakupendeza

Sauli aliungwa mkono na jeshi lake katika kuendeleza mapigano.

Hebu na tumkaribie Mungu mahali hapa

"kumkaribia Mungu" ni kitendo cha kutaka ushauri kwake. " hebu tumuulize Mungu la kufanya"

utawaweka katika mkono wa Israeli

"utatusaidia kuwashinda"

Lakini Mungu hakumjibu siku hiyo

Hii inadhihirisha kuwa Mungu hakuwa tayari kumsaidia Sauli.

1 Samuel 14:38

mjue na kuona jinsi dhambi hii ilivyotokea leo

"mjue nani aliyefanya dhambi"

Watu

Hawa ni Waisraeli.

hata kama angekuwa mwanangu Yonathani, atapaswa kufa

Sauli alisema hivi kwa sababu hakuamini kuwa mwanaye Yonadhani alikuwa na makosa.

akini hakuna hata mtu mmoja miongoni mwa watu aliye mjibu neno.

Watu walikuwa kimya kwa sababu wengi wao walijua kuwa Yonathani alivunja kiapo cha Sauli.

1 Samuel 14:40

Basi akawaambia Waisraeli wote

"Akawaambia askari wa Israeli waliokuwepo hapo"

Tuoneshe Thumimu ... wakatwaliwa ... piga kura

Wakati huo Waisraeli walitumia wawe maalumu yaliyoitwa Urimu na Thumimu katika kupokea maelekezo toka kwa Mungu.

1 Samuel 14:43

Taarifa ya jumla:

Kura ilionesha kuwa Yonathani alitenda dhambi.

Niambie umefanya nini

"Niambie ni kwa namna gani umetenda dhambi" au "niambie ni kosa gani umefanya"

Nitakufa

Yaweza kuwa na maana ya 1) "nipo tayari kufa" au 2) "Je nina sitahili kufa kwa sababu ya nilichokifanya"

Mungu afanye hivyo na kuzidi hata kwangu, kama Yonathani hautakufa

Sauli alifanya tena kiapo kibaya. "Mungu na aniue kama sitakuua wewe Yonathani"

1 Samuel 14:45

Taarifa ya jumla:

Jeshi linamtetea na kumlinda Yonathani toka kwa Sauli.

Je, inampasa Sauli afe, ni nani aliyetekeleza ushindi huu mkubwa kwa ajili ya Israeli? Mbali na hayo

"Yonathani amekamilisha ushindi huu mkubwa. Hakika hatakufa"

Kama Bwana aishivyo

Watu wanaonesha uhakika wao kuwa hawataruhusu lolote limpate Yonathani.

hata unywele mmoja wa kichwa chake hautaanguka chini

Hii inaonesha kuwa Watu wa Israeli watamlinda Yonathani. "tutamlinda na mabaya yote"

1 Samuel 14:47

Taarifa ya jumla:

Kwa muda mfupi Sauli aliwapiga maadui wa Israeli.

Israeli

Israeli inawakilisha watu wa Israeli.

Moabu

Hii inawakilisha watu wa Moabu.

Edomu

Hii inawakilisha watu wa Moabu.

Popote alipogeukia

"popote alipotuma jeshi lake"

kutoka kwenye mikono

"kutoka kwenye utawala"

1 Samuel 14:49

Taarifa ya jumla:

Hii inaonesha taarifa ya familia ya Sauli.

Ishvi ... Malkishua

Haya ni majina ya wanaume.

Merabu ... Mikali

Haya ni majina ya wanawake.

Ahinoamu ... Ahimaasi

Haya ni majina ya wanawake.

Abneri ... Neri ... Kishi ... Kishi

Haya ni majina ya wanaume.

1 Samuel 14:52

Siku zote za Sauli

"maisha yote ya Sauli"

alimuunganisha kwake

"alimlazimisha kujiunga na jeshi lake"

1 Samuel 15

1 Samuel 15:1

Maneno ya Bwana

"ujumbe wa Bwana"

ukaangamize kabisa vitu vyote walivyo navyo ... ua wote mwanamme na mwanamke, mtoto na mtoto mchanga, ng'ombe na kondoo, ngamia na punda

Sentensi hizi zina maana moja. Sentensi ya pili inaelezea kwa undani vitu ambavyo vinapaswa kuharibiwa.

Usiwaache

Hii inasisitiza kuharibu kila kitu.

1 Samuel 15:4

Watu

"jeshi"

kuwahesabu

"kuwahesabu"

mji wa Talemu

Mji ulioko kusini mwa Yuda.

watu mia mbili elfu waendao kwa miguu, na watu elfu kumi kutoka Yuda

watu 200,000 waendao kwa miguu, na watu 10,000 kutoka Yuda

1 Samuel 15:6

Wakeni

Kundi la wafugaji ambalo walikuwa marafiki wa taifa la Israeli.

Havila ... Shuri

Haya ni majina ya mahali.

1 Samuel 15:8

Taarifa ya jumla:

Sauli anapuuzia maeneo ambayo Bwana aliagiza yaangamizwe.

akamchukua Agagi

"akamkamata Agagi"

ncha ya upanga

"ncha ya upanga" inawakilisha jeshi la taifa la Israeli.

Sauli ... wakamwacha Agagi

Sauli hakumtii Mungu kwa kumuacha Agagi aishi.

pamoja na kondoo wazuri

Sauli hakumtii Mungu kwa kuchukua wanyama wazuri.

Hawakuangamiza

"waliviweka kwa ajili yao wenyewe"

1 Samuel 15:10

Neno la Bwana likamjia

"Bwana akasema maneno yake"

Neno la Bwana

"ujumbe wa Bwana"

Inanihuzunisha

"Nina huzuni"

aligeuka nyuma asinifuate

"Aliacha kunifuata"

hakutekeleza maagizo yangu

"hakutii yale niliyomuamuru ayafanye"

Samweli alikasirika

Samweli alikasirika kwa sababu ya kutotii kwa Sauli.

1 Samuel 15:12

Samweli aliambiwa

"mtu alimwambia Samweli"

amejijengea ukumbusho kwa ajili yake

Sauli alikuwa na kiburi

chini hadi Gilgali

Gilgali ilikuwa chini zaidi ya Karimeli.

nimetekeleza amri ya Bwana

Haipo wazi ikiwa Sauli anaelewa kuwa hakutii amri ya Mungu ya kuwaangamiza kabisa Waamaleki.

1 Samuel 15:14

Taarifa ya jumla:

Samweli anauliza kwa nini Sauli hakuwaangamiza kabisa Waameleki.

masikioni mwangu ... ninayosikia

Maneno haya yana maana sawa. "masikioni mwangu" ina maana ya "kusikia"

kilio cha kondoo ... milio ya ng'ombe

Hii ni milio ambayo wanyama hutoa. Lugha yako yaweza kuwa na maneno tofauti.

Wao wamewaleta ... watu waliwaacha

Watu hawa wanaozungumziwa hapa ni jeshi la Sauli.

Sadaka kwa Bwana Mungu wako

Sauli anajitetea kuwa wanyama kwa ajili ya dhabihu walikuwa sababu ya kutotii amri ya Bwana ya kutoangamiza kila kitu.

Bwana Mungu wako

Sauli hapa hamuelezei Mungu wa Samweli kama Mungu wake mwenyewe.

1 Samuel 15:17

machoni pako mwenyewe

"kwa mawazo yako mwenyewe"

je, hukufanywa mkuu wa kabila za Israeli?

Samweli anatumia swali hili kumueleza Sauli ni vitu vingapi Mungu amempa. "Mungu amekufanya kuwa mtawala wa kabila za Israeli"

Kwa nini basi haukuitii ... ukafanya uovu machoni pa Bwana?

Samweli anauliza swali hili kwa kumkemea Sauli kwa kutomtii Mungu.

Sauti ya Bwana

"Vitu ambavyo Bwana ameamuru"

bali badala yake ulishikilia nyara

Samweli anamshitaki Sauli moja kwa moja kwa kutokutii.

Nyara

"Nyara" ni vitu unavyovichukua toka kwa adui.

Uovu machoni pa Bwana

"ambayo Bwana anayaona kuwa ni uovu"

1 Samuel 15:20

Kweli kabisa niliitii sauti ya Bwana.

Sentensi hii haipo wazi kama Sauli alifikiri kuwa hili ni kweli au alikuwa akijitetea kwa sababu ya dhambi yake.

Sauti ya Bwana

"Vitu ambavyo Bwana ameamuru"

Lakini watu walichukua

Hapa anahamisha lawama kwa watu.

vitu vilivyokusudiwa kuangamizwa

Wanyama ambao Bwana aliamuru waharibiwe"

Gilgali

Hili ni jina la mahali.

Agagi

Hili ni jina la mfalme wa Waameleki.

1 Samuel 15:22

Je, BWANA hufurahia sadaka za kuteketezwa na dhabihu kama ilivyo kuitii sauti yake?

Samweli alitumia swali hili kusisitiza kuwa kutii ni jambo la muhimu sana kuliko dhabihu.

Sauti ya Bwana

"Vitu ambavyo Bwana ameamuru"

Utii ni bora kuliko dhabihu

Mungu alitaka Sauli amtii kabisa kwa kuwaangamiza Waamaleki. Hakuna kilichokuwepo kwenye nchi ambacho kilifaa kwa dhabihu.

bora kuliko mafuta ya beberu

"bora kuliko dhabihu ya mafuta ua beberu kama sadaka ya kuteketezwa"

uasi ni sawa na dhambi ya uchawi

"uasi ni kama dhambi ya kufanya uchawi"

ukaidi ni sawa na uovu na udhalimu

"Kuwa mkaidi ni sawa na dhambi ya kuabudu sanamu"

umelikataa neno la Bwana

"umekataa kufanya jambo ambalo Bwana ameamuru"

amekukataa usiwe mfalme

"ameamua kuwa hautakuwa tena mfalme"

1 Samuel 15:24

nimevunja amri ya BWANA

"Sikutii aliloliamuru Bwana"

kwa sababu niliwaogopa watu

"Kwa sababu niliwaogopa askari"

kuitii sauti yao

"kufanya kile walichokiomba"

urudi nami

Sauli na Samweli walikuwa waliongea faragha mbali na watu wengine.

1 Samuel 15:26

kwa sababu umekataa neno la BWANA

Samweli anaonesha wazi kuwa Sauli ameelewa kuwa hakumtii Bwana wakati ambapo waliwaacha wanyama wazuri na hakumuua Agagi.

Umekataa neno la Bwana

"Umekataa kufanya aliloliamuru Mwana"

Sauli akashika pindo la kanzu yake

Sauli alifanya hivi ili kumzuia Samweli asiondoke.

pindo la kanzu yake

"mwisho wa kanzu yake"

1 Samuel 15:28

Bwana ameuchana ufalme wa Israeli

"Kama ulivyochana kanzu yangu vivyo hivyo Bwana ameuchana ufalme wa Israeli"

amempa jirani yako, aliye bora kuliko wewe.

Mungu ameshaamua ni nani atakuwa mfalme baada ya Sauli.

Uwezo wa Israeli

Hii inamuelezea Mungu ambaye huwapa nguvu Waisraeli.

hatasema uongo wala kubadili nia yake

Hii inasisitiza kuwa Mungu hasemi uongo.

nia yake

"alichoamua kukifanya"

si mwanadamu, kwamba abadili nia yake

"Yeye ni Mungu na atafanya alichosema kuwa atakifanya"

1 Samuel 15:30

Lakini tafadhali nipe heshima wakati huu mbele ya wakuu

Sauli alikuwa anatamani sana kuheshimiwa na watu badala ya kumwabudu Mungu.

mbele ya wakuu wa watu wangu na mbele ya Israeli

"mbele ya watu wa Israeli na viongozi wanaowaongoza"

Urudi tena pamoja nami

"Urudi pamoja nami"

Hivyo Samweli akamrudia tena Sauli

Hii inaonesha kuwa Samweli alibadili mawazo yake na akarudi pamoja na Sauli walipokuwepo watu.

1 Samuel 15:32

Agagi akafika kwake akiwa amefungwa minyororo

"walimpeleka Agagi akiwa amefungwa minyororo"

Hakika uchungu wa kifo umepita

"Kwa hakika sipo tena katika hatari au kufa"

Jinsi upanga wako ulivyofanya wanawake wapoteze watoto, vivyo hivyo mama yako naye hatakuwa na mtoto miongoni mwa wanawake

Maneno haya yana maana moja "Kwa kuwa umewaua watu, wewe pia utauawa"

ulivyofanya wanawake wapoteze watoto, vivyo hivyo mama yako naye hatakuwa na mtoto

"umewaua watoto wa wanawake wengine, hivyo nitamuua mtoto wa mama yako"

Kisha Samweli akamkata Agagi vipande vipande

Samweli aliimaliza kazi ambayo Bwana alimuamuru Samweli alifanye.

1 Samuel 15:34

Rama ... Gibea

Haya ni majina ya mahali.

akapanda kwenda nyumbani kwake Gibea

Gibea ilikuwa juu kuliko Gilgali ambapo Sauli na Samweli walikuwa wakizungumza.

Samweli hakumuona tena Sauli hadi siku ya kifo chake

Hii inaonesha kuwa Samweli alikufa mbele ya Sauli lakini hakumuona Sauli tena kipindi akiwa hai.

1 Samuel 16

1 Samuel 16:1

Utamlilia Sauli kwa muda gani, ikiwa nimemkataa asiwe mfalme juu ya Israeli?

"Acha kumlilia Sauli niliyemkataa asiwe mfalme juu ya Israeli"

Ijaze pembe yako mafuta

Pembe ilitumika mara nyingine kama chupa. Chupa ya mafuta ilitumika kwa ajili ya kumpaka mafuta mfalme, kama Samweli alivyofanya kwa Daudi.

1 Samuel 16:2

Nitakwendaje?

Samweli anatumia swali kusisitiza kuwa anaogopa kwenda Bethlehemu.

pamoja nawe na usema

"pamoja nawe mpaka Bethlehemu na uzungumze na watu wa huko"

na useme, 'Nimekuja kutoa dhabihu kwa BWANA

"na uwaambie watu wa huko kuwa umekwenda kutoa dhabihu kwa Bwana"

1 Samuel 16:4

Wazee wa mji walikuwa wakitetemeka walipokuja kuonana

Wazee walikuwa wakitetemeka kwa sababu waliogopa kuwa Samweli amekwenda kuwakemea.

Kwa amani

"ndio, nimekuja kwa amani"

Jitoeni wenyewe

"Kujitoa" inamaana ya kuwa watu wajitoe wenyewe tayari kwa ajili ya kusudi la Mungu kwa kujitakasa kutokana na sheria ya Musa.

1 Samuel 16:6

Walipofika

"Hawa ni Yese na watoto wake"

akamwangalia Eliabu

Samweli alimuangalia Eliabu.

Eliabu

Hili ni jina la moja wa wana wakubwa wa Yese.

amesimama mbele yake

Mbele ya Bwana.

Bwana haangalii kama mtu aangaliavyo.

"Kuangalia" ina maana ya kutathimini jambo.

Kwa kuwa Bwana haangalii ... Bwana anaangalia

"Kwa kuwa mimi Bwana siangalii ... Mimi Bwana naangalia"

Moyo

"Moyo" inawakilisha sehemu ya ndani ya mtu.

1 Samuel 16:8

Abinadabu ... Shama

Haya ni majina ya wana wa Yese.

akamwambia apite mbele ya Samweli

"Akamwambia aende kwa Samweli"

Kisha Yese akmwambia Shama apite

"Kisha Yese akamwambia Shama aende kwa Samweli"

1 Samuel 16:11

Yupo mdogo kabisa amesalia

"Bado yupo mtoto wangu mdogo"

hatutakaa chini

"Hatutakaa chini ili tule"

Naye ... muonekano

Hapa msimuliaji anatusimulia kuhusu mtu mwingine katika simulizi.

kijana huyu alikuwa mwekundu

Hii inamaanisha kuwa Daudi alikuwa na mwonekano wenye afya.

1 Samuel 16:13

pembe yenye mafuta

Pembe ilitumika mara nyingine kama chupa. Chupa ya mafuta ilitumika kwa ajili ya kumpaka mafuta mfalme, kama Samweli alivyofanya kwa Daudi.

Samweli akanyanyuka na kwenda

Hii inaonesha kuwa alinyanyuka baada ya kukaa na kula.

Roho wa Bwana akamwijia Daudi

Roho wa Bwana alimchochea Daudi. Roho wa Bwana alimuwezzesha Daudi kutimiza yote ambayo Bwana alimtaka ayafanye.

1 Samuel 16:14

Basi

Hapa msimuliaji anaanza kutuambia sehemu mpya ya simulizi.

roho ya ubaya kutoka kwa Bwana

"roho ya ubaya" ni "roho inayosababisha matatizo"

Haya bwana wetu hebu sasa amuru

Watumishi wanamchukulia Sauli kama bwana wao.

amuru watumishi wako walio mbele yako wamtafute

"tuamuru sisi watumishi wako tunaokutumikia tumtafute"

yuko juu yako

"anakusumbua wewe"

1 Samuel 16:17

mwenye nguvu, mtu jasiri

Yaweza kuwa na maana ya 1) "shujaa" au 2) "mtu mwenye hekima"

mwenye busara aongeapo

"anayeongea kwa busara"

Bwana yuko pamoja naye

Hii inamaanisha kuwa Bwana alimsaidia na kumbariki Daudi.

1 Samuel 16:20

Daudi akafika kwa Sauli

"Daudi akaenda kwa Sauli.

kuanza kazi yake

"na akaanza kumtumikia"

akawa mbeba silaha wake

Daudi akawa mbeba silaha wa Sauli.

1 Samuel 16:22

Mruhusu Daudi awe mbele yangu

"Kusimama mbele yangu" inamaanisha kuwa aendelee kumtumikia Sauli"

amepata kibali machoni pangu

"Nimependezwa naye"

Roho ya ubaya kutoka kwa Bwana.

"roho ya ubaya" ni "roho inayosababisha matatizo"

kiwapo juu ya Sauli

Ikamsumbua Sauli"

Sauli angeburudishwa na kupona

"Muziki ungemfurahisha Sauli na kumfanya ajisikie vizuri"

1 Samuel 17

1 Samuel 17:2

bonde la Ela

Hili ni jina la bonde.

1 Samuel 17:4

mikono sita na shubiri moja

Mkono mmoja ni sawa na sentimeta 46. Shubiri ni sawa na urefu wa sentimeta 23.

alivaa dirii ya chuma

"alijilinda mwenyewe kwa kuvaa dirii ya chuma"

Shekeli elfu tano

Shekeli ni kama ujazo wa gramu 11.

1 Samuel 17:6

mkuki wa shaba

Huu ni mkuki mdogo ambao upo kwa aliji ya kurushwa.

mpini wa mkuki wake

"mshikio wa mkuki wake"

kamba ya sindano ya mfumaji

"kamba inayozunguka"

Kichwa cha mkuki wake

"Mwanzoni wa mkuki wake"

shekeli mia sita

Yapata kilogramu 7"

1 Samuel 17:8

Kwa nini mmekuja na mmejipanga kwa ajili ya vita?

"kwa nini mmekuja kupigana dhidi yetu?" Goliati alitumia swali hili ili kuwadhihaki Waisraeli.

Mimi si Mfilisti, na ninyi si watumishi wa Sauli?

Goliati alitumia swali hili ili kuwadhihaki Waisraeli. "Mimi ni Mfilisti mkuu na ninyi ni watumishi wa Sauli"

1 Samuel 17:10

Leo ninayapa changamoto majeshi ya Israeli

"Ninalipa changamoto jeshi wa Israeli"

Israeli wote

Hawa ni askari wa Israeli waliokuwepo huko.

walikata tamaa na kuogopa sana

Maneno haya yanamaana moja ya kuonesha walikuwa na hofu kuu.

1 Samuel 17:12

alikuwa na watoto wanane

Hapa anazungumziwa Yese.

Yese alikuwa mzee ... mzee mwenye umri mkubwa

Maneno haya yanaonesha msisitizo mkubwa.

aliyemfuata Abinadabu, na watatu aliitwa Shama

"Abinadabu alikuwa mtoto wa pili na Shama alikuwa wa tatu.

1 Samuel 17:14

wakubwa watatu

"Wana wakubwa watatu wa Yese"

Kwa siku arobaini

"kwa siku 40"

akajitokeza kwa ajili ya vita

"akajitokeza kuwa yupo tayari kwa ajili ya vita"

1 Samuel 17:17

Efa

Efa ni kipimo sawa na lita 22.

jemedari kikosi chao cha elfu

Jeshi liligawanyika katika makundi ya watu elfu na kila kundi kilikuwa na jemedari.

Ukawaangalie wako na hali gani

"kaangalie na uone kaka zako wanaendeleaje"

1 Samuel 17:19

Watu wote wa Israeli

"askari wote wa Israeli"

bonde la Ela

Hili ni jina la bonde.

1 Samuel 17:22

jina lake Goliathi

"Ambaye jina lake aliitwa Goliati"

akajitokeza kutoka majeshi ya Wafilisti

"akatokeza mbele toka kwa jeshi la Wafilisti"

1 Samuel 17:25

Umemuona mtu huyu aliyejitokeza?

"Muangalie mtu huyu aliyejitokeza"

Mfalme

"mfalme wetu"

Binti yake

Huyu ni binti wa mfalme.

atampa ... nyumba ya baba yake

Huyu ni mtu atakayemuua Goliati.

ataifanya familia ya baba yake isilipe kodi katika Israeli.

"hataruhusu familia yake ilipe kodi"

1 Samuel 17:26

kuiondolea Israeli fedheha

"na akaifanya Israeli isifedheheke tena"

Ni nani Mfilisti huyu asiyetahiriwa ayatukanaye majeshi ya Mungu aliye hai?

Daudi alisema maneno haya kuonesha hasira yake kwa Wafilisti wanaolidharau jeshi la Mungu.

Mfilisti huyu asiyetahiriwa

Maneno haya yanaonesha kuwa Goliati hakuwa mtu wa Mungu aliye hai.

1 Samuel 17:28

Hasira ya Eliabu ikawaka moto dhidi ya Daudi

Hapa hasira inafananishwa na moto uwakao.

Kwa nini umekuja hapa?

Eliabu anatumia swali hili kuonesha kuwa alikuwa na hasira na Daudi.

Wale kondoo wachache umewaacha na nani huko nyikani?

Eliabu alitumia swali hili kwa kumdhihaki Daudi kwa kuonesha kuwa kazi yake haikuwa ya muhimu na kumuhukumu kwa kutokuangalia kondoo wa baba yake.

kiburi chako, na utundu wa moyo wako

Maneno haya yanaonesha msisitizo.

"Nimefanya nini sasa? Mimi si numeliuliza swali tu?

"Sijafanya jambo lolote baya, nilikuwa nauliza swali tuu"

Akamgeukia na kumuacha

Hapa Daudi aligeuka na kumuacha Eliabu.

1 Samuel 17:31

Maneno aliyosema Daudi yaliposikika

"Askari waliposikia aliyoyasema Daudi"

Pasiwepo moyo wa mtu atakayezimia

"asiwepo mtu atakayepoteza ujasiri"

Mtumishi wako atakwenda

"Mimi mtumishi wako nitakwenda"

1 Samuel 17:34

Mtumishi wako alikuwa akichunga kondoo za baba yake

Daudi anajizungumzia mwenyewe kama "mtumishi wako" kuonesha heshima kwa Sauli.

alikuwa akichunga kondoo za baba yake

"alikuwa akitunza kondoo wa baba yake"

dubu

Dubu ni mnyama mkubwa mwenye miguu minne lakini anaweza kusimama na miguu miwili kama mtu.

Nilimfukuza na kumshambulia

Hapa anazungumziwa simba au dubu.

na kumpokonya kutoka kinywani mwake

Hapa anazungumziwa mwana kondoo.

aliponirukia

"alinivamia"

nilimshika ndevu zake

"ndevu" zinamuelezea simba au nywele zilizopo katika uso wa dubu.

1 Samuel 17:36

Sentensi unganishi

Daudi anaendelea kuzungumza na mfalme Sauli.

Mfilisti asiyetahiriwa

Maneno haya yanaonesha kuwa Goliati hakuwa mtu wa Mungu aliye hai.

atakuwa kama mmoja wao

Daudi ataweza kumuua Mfilisti kama alivyoweza kumuua simba na dubu.

1 Samuel 17:37

kutoka makucha ya simba na makucha ya dubu

Simba na dubu hutumia kucha zao kuvamia hivyo "kucha" inawakilisha kuvamia.

mkono wa Mfilisti

"nguvu za Mfilisti huyu"

chepeo ya shaba

Vazi la kivita lililofunikwa kwa mabamba madogo.

1 Samuel 17:39

upanga wake juu ya vazi lake

"upanga wa Sauli juu ya vazi lake"

fimbo mkononi mwake

Hapa anamuelezea Daudi.

Kombeo lake lilikuwa mkononi mwake

Kombeo ni silaha iliyotumika kwa ajili ya kurusha mawe.

1 Samuel 17:41

mbeba ngao yake akiwa mbele yake.

"na mbeba ngao yake alikuwa mbele yake"

akamdharau

"akamchukia"

mwekundu

"mwenye afya"

Je, mimi ni mbwa, hata ukanijia na fimbo?

Mbwa anawakilisha mnyama mdogo ambaye mtu anaweza kumuua kwa urahisi. "Umenidharau kwa kunujia kwa fimbo kama vile nimekuwa mbwa"

1 Samuel 17:44

nyama yako nitawatupia ndege wa angani na wanyama wa mwituni

Goliati anazungumzia kumuua Daudi na kuacha mwili wake chini kwa ajili ya kuliwa na wanyama kama vile kuutoa mwili wa Daudi ili uliwe na wanyama.

Ndege wa angani

"ndege"

wanyama wa mwituni

"wanyama wa porini"

Kwa jina la Bwana

"kwa nguvu ya Bwana" au "kwa mamlaka ya Bwana"

uliyemdharau

"uliyemdhihaki"

1 Samuel 17:46

Sentensi unganishi:

Daudi anaendelea kuaongea na Goliati.

Nitawapa mizoga ... ndege ... na wanyama wa mwituni

Daudi anaongea katika kuwaongoza Waisraeli kuwaua Wafilisti na kuacha maiti zao katika ardhi ili wanyama wale. "Tutawaua Wafilisti na ndege wa angani na wanyama wa mwituni watawala"

dunia yote ijue

"watu wote wa duniani wajue"

Bwana hatui ushindi kwa upanga wala mkuki

Panga na mkuki ni silaha za vita. "Ushindi anaoutoa Bwana hautegemei upanga wala mkuki"

Vita ni ya Bwana

"Bwana huwa anashinda vita wakati wote"

atawaweka katika mkono wetu

"atatusaidia kuwashinda"

1 Samuel 17:50

Daudi alimshinda ... Alimpiga ... kumuua ... Mkononi mwa Daudi hakukuwa na upanga

Mstari wa 50 unaonesha ushindi wa pekee wa Daudi juu ya Goliati. Inaonesha namna ambavyo Daudi alimuua Goliati.

Ndipo Daudi akakimbia akasimama juu ya Mfilisti

Daudi alifanya hivi baada ya Goliati kuanguka chini.

Akachukua upanga wake

"akachukua upanga wa Mfilisti"

1 Samuel 17:52

Na maiti za Wafilisti walilala katika njia iendayo Shaaraimu

"Na wakawaua Wafilisti na maiti za Wafilisti katika njia iendayo Shaaraimu"

wakateka nyara kambi yao

"Waisraeli waliteka nyara kambi za Wafilisti"

akaliweka vazi la vita katika hema lake

"akaweka vazi la vita la Goliati katika hema yake"

1 Samuel 17:55

Sauli alipomuona Daudi

Mazungumzo katika 17:55-56 yalitokea kabla Daudi hajamuua Goliati.

akienda kukabiliana na yule Mfilisti

"akienda kupigana na Mfilisti"

kijana huyu ni mtoto wa nani

"baba yake na huyu kijana ni nani"

Kama uishivyo

Hii ni namna ya kuapa na kuonesha kuwa anayotaka kuyasema ni kweli.

mvulana huyu ni kijana wa nani

"baba yake na kijana huyu ni nani"

1 Samuel 17:57

mkononi mwake

Hapa anazungumziwa Daudi

wewe ni mtoto wa nani?

"Baba yako ni nani"

Mimi ni mtoto wa mtumishi wako Yese Mbethlehemu

"Baba yangu ni mtumishi wako Yese Mbethlehemu"

Mtumishi wako Yese

Daudi anatumia neno hili "mtumishi wako" kuonesha kuwa baba yake alikuwa mwaminifu kwa mfalme Sauli.

1 Samuel 18

1 Samuel 18:1

roho ya Yonathani ilishikana na roho ya Daudi

Urafiki wa karibu sana unasemwa kama unavyounganisha roho za watu wawili. Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "Yonathani alipenda sana Daudi' au 'Yonathani alijitolea kwa Daudi"

Yonathani akampenda kama roho yake mwenyewe

Hapa "kupendwa" inaonyesha upendo kati ya marafiki, si upendo wa kimapenzi. Neno "nafsi" linawakilisha mtu au maisha ya mtu. AT "Yonathani alipenda Daudi kama alivyojipenda mwenyewe" au "Yonathani alipenda Daudi kama alipenda maisha yake mwenyewe"

1 Samuel 18:3

Yonathani akampenda kama roho yake mwenyewe

Hapa "kupendwa" inaonyesha upendo kati ya marafiki, si upendo wa kimapenzi. Neno "nafsi" linawakilisha mtu au maisha ya mtu. Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 18:1. Wakati "Yonathani alipenda Daudi kama alivyojipenda mwenyewe" au "Yonathani alipenda Daudi kama alipenda maisha yake mwenyewe"

1 Samuel 18:5

naye alifanikiwa

"naye alifanikiwa"

Jambo hili lilipendeza machoni pa watu na katika macho ya watumishi wa Sauli.

Maneno "mbele ya" na "mbele ya" yanamaanisha kitu kimoja. Maoni ya watu yanasemwa kuwa kitu ambacho wanachokiona kama kizuri au mbaya. AT "Hii ilikuwa ya kupendeza katika maoni ya watu wote na watumishi wa Sauli" au "Hii iliwafaidi watu wote na watumishi wa Sauli"

1 Samuel 18:6

kutoka miji yote ya Israeli

Hii ni kufanya kusisitiza idadi kubwa ya wanawake waliokuja. AT "kutoka miji mingi katika Israeli"

wakiwa na matowazi, wenye furaha, na wakiwa na ala za muziki

"kucheza matowazi kwa furaha na ala za muziki"

wakiwa na matowazi

"matowazi" ni ngoma ndogo ya mkono

Na Daudi ameua makumi elfu yake

Kitenzi kinaweza kutolewa kutoka kwenye mstari uliopita. AT "na Daudi ameua makumi elfu"

1 Samuel 18:8

Wamemsifia

"Wameshukuru"

Atapata kitu gani zaidi isipokuwa ufalme?

Swali hili la uongo linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Kitu pekee ambacho anahitaji ni ufalme."

1 Samuel 18:10

roho ya ubaya kutoka kwa Mungu

Hapa "roho ya ubaya" inaweza kutaja "roho inayosababisha shida" au "roho ya ubaya." Tazama jinsi ulivyotafasiri hii katika 16"14.

roho ya ubaya kutoka kwa Mungu ikamwingia Sauli

Maneno "ikamuingia" yanamaanisha roho ya madhara yalisaidia Sauli. Katika kesi hii ina maana kwamba umesababisha Sauli kuwa na wasiwasi na kutenda mambo. Tazama jinsi ulivyotafasiri maneno sawa katika 10:5.

na akachukiza

"Naye akajifanya kichaa"

Bwana alikuwa pamoja nae

"Bwana alikuwa pamoja na Daudi"

1 Samuel 18:13

Hivyo Sauli alimuondoa Daudi mbele yake

"Basi Sauli akamwondoa Daudi kuondoka mbele yake"

maelfu

Hii inaweza kuwakilishwa kwa nambari. AT "watu 1,000"

David alitoka na kuingia mbele ya watu

Hapa "watu" hutaja askari chini ya amri ya Daudi. Maneno ambayo "kutoka" na "kuingia" ni maadui ambayo inahusu kuwaongoza watu katika vita na kuwaongoza nyumbani kutoka vita. AT "Daudi aliwaongoza askari wake katika vita na kuwaongoza nyumbani kutoka vita"

1 Samuel 18:15

alimwogopa

Hapa "kumwogopa" ni maneno ambayo ina maana ya hofu. AT "alimwogopa Daudi"

watu wote wa Israeli na Yuda walimpenda Daudi

Hapa "Israeli na Yuda" wanawakilisha watu wa kabila zote. AT "watu wote wa Israeli na Yuda walimpenda Daudi"

alitoka na kuingia mbele yao

Maneno ambayo "toka" na "ingia" ni maneno ambayo yanahusu kuwaongoza watu katika vita na kuwaongoza kwenda nyumbani kutoka vitani. Tazama jinsi ulivyotafasiri hii katika 18:13. AT "aliongoza askari wake katika vita na kuwaongoza nyumbani kutoka vitani"

1 Samuel 18:17

Usije mkono wangu ukawa juu yake, ila acha mkono wa Wafilisti uwe juu yake

Kumharibu mtu kunazungumzwa kama kuwachini ya mtu huyo. Hapa, Sauli anataja kumwua Daudi. AT "Mimi sio nitakaye kumwua; Nitawawezesha Wafilisti kumwua"

Mimi ni nani, na maisha yangu yana nini, au hata maisha ya familia ya baba yangu katika Israeli......kwa mfalme?

Daudi hutumia swali hili la kuvutia ili kusisitiza kuwa hastahili kuwa mkwe wa Sauli. AT "Mimi si mtu na jamaa zangu wala familia ya baba yangu ni muhimu sana kwa Israeli ... kwa mfalme."

mkwe wa mfalme

mkwe wa mfalme - "mume wa binti ya mfalme"

1 Samuel 18:19

wakati Merabu, binti ya Sauli, angepaswa kupewa Daudi

Hii inaweza kuelezwa katika fomu harisi. AT "wakati Sauli angempati Daudi binti yake Merabu"

aliozwa kwa Adrieli

Hii inaweza kuelezwa katika fomu harisi. AT "Sauli akampa Adrieli"

1 Samuel 18:20

Mikali.... alimpenda Daudi

Hapa "kupendwa" maana yake alikuwa na hisia za kimapenzi kwa Daudi.

Akamuambia Sauli

Hapa "wao" inahusisha watu ambao walijua kuhusu hisia za Mikali, si kwa Daudi na Mikali.

hivyo mkono wa Wafilisti pengine uwe juu yake

Kumharibu mtu kunazungumzwa kama kunaweka mtu chini ya mwingine. Hapa, Sauli akimaanisha kumwua Daudi. Tazama jinsi ulivyotafasiri maneno sawa katika 18:17. AT "ili Wafilisti wasimwue"

Wewe utakuwa mkwe wangu

mkwewe - "utakuwa mume wa binti yangu"

1 Samuel 18:22

watumishi wake wote wanakupenda

"watumishi wake wote wanakubali"

Sasa basi

"Kwa sababu hizi unapaswa"

1 Samuel 18:23

Kwenu ninyi mnaona ni jambo dogo kuwa mkwe wa mfalme, mimi ni maskini, na heshima yangu ni ndogo?

mkwe, kwani mimi ni mtu maskini, na ninahesabiwa kidogo? - Daudi anauliza swali hili la kuvutia ili kusisitiza kuwa hastahili kuwa mkwe wa mfalme. AT "Ni jambo kubwa kuwa mkwe wa mfalme, na mimi ni maskini sana na si muhimu kwa hilo."

1 Samuel 18:25

'Mfalme haitaji mahari yoyote, isipokuwa govi mia moja

Kitenzi cha maneno ya pili inaweza kutolewa kutoka kwa ya kwanza. AT "Mfalme hataki zawadi yoyote; anahitaji tu kwamba unamletea govi 100"

govi

"mahali". Katika utamaduni huu, mtu huyo alihitajika kutoa zawadi kwa baba mkwe.

govi

Neno "govi" linamaanisha ngozi ya kwenye sehemu za siri ambayo inaondolewa wakati wa kutahiriwa.

ili ajilipize kisasi kwa adui wa mfalme

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "kulipiza kisasi juu ya maadui wa mfalme"

kumfanya Daudi kuangukia kwenye mikono ya Wafilisti

Hapa "kuanguka" maana yake kufa. Neno "mkono" linawakilisha Wafilisti. Hii inaweza kuelezwa katika fomu harisi. AT "Wafilisti kumuua Daudi"

1 Samuel 18:27

Wafilisti mia mbili

Hii inaweza kutafsiriwa kwa nambari. AT "200 Wafilisti"

kumkadhi mfalme kulingana na idadi yake

"Daudi na watu wake wote waliwapa mfalme"

Sauli akaona, na akajua

Hapa maneno "kuona" na "kujua" yanashiriki maana sawa na kusisitiza kwamba Sauli alijua kwa uhakika. AT "Sauli alijua"

Mikali, binti Sauli, akampenda

Hapa "kupendwa" maana yake alikuwa na hisia za kimapenzi kwa Daudi.

1 Samuel 18:30

hivyo jina lake likapata heshima kubw

Hapa "jina" ni msamiati kwa Daudi. Hii inaweza kuelezwa katika fomu harisi. AT "ili watu wamheshimu sana Daudi"

1 Samuel 19

1 Samuel 19:1

watumishi wake wote

Hapa "wake" inamhusu Sauli.

alimfurahia sana Daudi

Yonathani alifurahi sana kuwa na Daudi.

1 Samuel 19:4

Mfalme asije akafanya dhambi dhidi ya mtumishi wake

Yonathani anaongea kama Sauli ni mtu mwingine kuonyesha Sauli kwamba Yonathani anamheshimu Sauli. AT "Usitende dhambi dhidi ya mtumishi wako"

alijitoa maisha yake

Hapa "kujitoa maisha yake" ni idiom ambayo inahusu kuhatarisha maisha yake. AT "alihatarisha maisha yake"

Kwa nini utende dhambi juu damu isiyo na hatia kwa kumuua Daudi bila sababu?

Yonathani anauliza swali hili kumkemea Sauli. Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "hupaswi kutenda dhambi dhidi ya damu isiyo na hatia na kumwua Daudi bila sababu."

dhambi juu damu isiyo na hatia

Hapa "damu" ni muhimu kwa maisha ya mtu asiye na hatia. AT "kufanya dhambi ya mauaji"

1 Samuel 19:6

yeye hatauawa

Hii inaweza kuelezwa katika fomu harisi. AT "Sitamwua" au "Sitamwua" au "Nitamfanya awe hai"

alikuwa mbele yake

Daudi alikuwa mbele ya Sauli.

1 Samuel 19:8

Yule roho mchafu kutoka kwa Bwana

Hapa "roho mchafu" inaweza kutaja 'roho inayosababisha shida" au "roho mchafu." Tafsiri kama katika 16:14.

1 Samuel 19:10

kumpigilia Daudi ukutani kwa mkuki

kutupa mkuki wake uweze kupita kwa Daudi na kwenye ukuta

anaweza kumwua

"Sauli anaweza kumwua Daudi"

Mikali.... akamuambia

Mikali alimwambia Daudi

Usipoyaokoa maisha yako

Hapa "Usipoyaokoa maisha yako" ni tendo ambalo linahusu kutoroka. AT "Ikiwa hutatoroka"

utauwawa

Hii inaweza kuelezwa katika fomu harisi. AT "mtu atakuua"

1 Samuel 19:12

Taarifa ya jumla

Mikali anamsaidia Daudi kumtoroka Mfalme Sauli. Anatumia sanamu ili kuonekana kwamba Daudi aonekane kuwa amelala kitandani.

akaweka mto wa singa za mbuzi kichwani pake, na akakifunika na nguo

Inawezekana maana ni 1) kichwa cha sanamu kilikuwa kimelala mto wa nywele za mbuzi na Mikali amevaa sanamu katika nguo za Daudi au 2) Mikali alitumia nguo za Daudi kama kifuniko ili kufunika kabisa sanamu na akafanya "mto" wa nywele za mbuzi kuonekana kama nywele za Daudi zikidondoka chini ya blangeti ya nguo.

1 Samuel 19:14

Taarifa za jumla

Sauli anaonyesha tamaa yake ya kumwua Daudi

akamchukua Daudi

'"akamrudisha Daudi kwa Sauli"

yeye akamuambia

Hapa "yeye" inamhusu Mikali.

Mleteni kwangu akiwa kitandani

Sababu kwa nini watu walidhani Daudi alikuwa kitandani inaweza kuwekwa wazi. AT "Ikiwa yeye ni mgonjwa sana hawezi kuja kwangu, uniletee akiwa kitandani"

1 Samuel 19:16

singa za mbuzi

Kama tafsiriwa katika 19:12.

tazama

Neno "tazama" hapa linaonyesha kwamba wajumbe walishangaa kwa kile walichoona.

Kwa nini umenidanganya na kumwachilia adui yangu aende, na tena ametoroka?

Maana iwezekanavyo ni 1) Sauli anataka kujua kwa nini Mikali alifanya kile alichofanya au 2) Sauli anatumia swali hili kumkemea Mikali. Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Wewe haukupaswa kunidanganya na kuruhusu adui yangu aende, kwa hiyo ametoroka."

Acha niende. Kwa nini nikuuwe?

Ijapokuwa Daudi hakuweza kusema, Mikali anamwambia Sauli kwamba Daudi alimtishia kwa swali hili. Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Mimi nitakuua ikiwa hunisaidia kuktoroka."

1 Samuel 19:18

Taarifa za jumla

Daudi anamkimbia Samweli.

Sasa

Neno hili linatumika hapa kuonyesha kwamba mwandishi ameanza kuongea sehemu mpya ya hadithi.

Nae Sauli akaambiwa

Hii inaweza kuelezwa katika fomu harisi. AT "Mtu alimwambia Sauli"

Tazama

"Angalia" au "Sikiliza" au "Jihadharini na kile ninachokuambia"

akisimama kama kiongozi wao

Hapa "kichwa" inahusu nafasi ya mamlaka. AT "akifanya kama kiongozi wao"

1 Samuel 19:21

Sauli alipoambiwa hivyo

Hii inaweza kuanza katika fomu harisi "Pale mtu alipomuambia Sauli hivyo"

Rama....Seku...Nayothi

Haya ni majina ya mahari

1 Samuel 19:23

Kwa sababu hii, wanasema, "Je! Sauli pia ni mmoja wa manabii?"

Hii ikawa miongoni mwa Waisraeli. Inaonekana watu walisema hii kueleza mshangao wakati mtu bila kutarajia alifanya kitu ambacho hakuwa amefanya kabla. Maana ya swali inaweza kuelezwa waziwazi. Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 10:11. AT "Hiyo ndio sababu wakati watu wanapoona mtu akifanya jambo ambalo haliwezekani, wanasema," Je! Sauli pia ni nabii"

wanasuliza

Hapa "wao" inahusu watu kwa ujumla. Swali lilikuwa maelekezo kati ya watu.

1 Samuel 20

1 Samuel 20:1

Nimefanya nini? Uovu wangu ni upi? Dhambi yangu ni ipi kwa baba yako, inayofanya atafute kuutoa uhai wangu

Maswali haya matatu yanamaanisha jambo sawa. Daudi anawatumia ili kusisitiza kwamba hakumfanyia chochote kibaya kwa Sauli. Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "sijafanya chochote kibaya. Sijafanya uovu wowote. Sijafanya dhambi dhidi ya baba yako. Yeye hana sababu ya kuchukua maisha yangu."

kwamba anataka kuutoa uhai wangu?

Hapa "kuchukua maisha yangu" ni maana ya "kuniua."

Mbali na hayo

Hapa "mbali na hayo" ni dhana inayoelezea kwamba si kweli. AT "Hii si kweli"

hakuna chochote kikubwa au kidogo

Maneno "kubwa au ndogo" yanajumuisha kila kitu katikati. AT "hakuna chochote"

Kwa nini inamlazimu baba yangu anifiche jambo hili?

Yonathani anatumia swali hili kusisitiza kwamba Sauli angemwambia kama angepanga kumwua Daudi. Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Baba yangu hana sababu ya kuficha jambo hili kwangu" au "Ikiwa jambo hili ni kweli, baba yangu hakika nitanijulishe"

La, siyo hivyo

"Si kweli"

1 Samuel 20:3

Nimepata kibali machoni pako

Hapa macho yanawakilisha kuona, na kuona inawakilisha mawazo au hukumu. AT "Nimekupendeza wewe" au "unaniona vizuri"

atakuwa mwenye huzuni

Hii inaweza kuelezwa katika fomu harisi. AT "hii itashuhudia yeye" au "atakuwa na huzuni sana"

kuna hatua moja tu kati yangu na mauti

Hapa "hatua kati yangu na mauti" ni msemo ambao unahusu kuwa karibu sana na mauti. AT "Mimi ni karibu sana mauti"

1 Samuel 20:4

Taarifa za jumla

Daudi anapendekeza jaribu dhidi ya Mfalme Sauli kwa Yonathani

Kesho ni siku ya mwezi mpya

Siku ya kwanza ya mwezi kila mwezi watu walisherehekea na kutoa sadaka kwa Mungu.

hadi siku ya tatu jioni

"mpaka jioni ya siku ya kesho"

1 Samuel 20:6

Sentensi Unganishi

Daudi anaendelea kuelezea jaribu analopendekeza.

aliuliza kuondoka kwangu

"aliniuliza kama nitamruhusu aondoke"

anasema ... yeye ni ... ameamua

Neno "yeye" linamaanisha Sauli.

mtumishi wako atakuwa na amani

Daudi anazungumza mwenyewe kama ni mtu mwingine kuonyesha kwamba anamheshimu Yonathani. AT "Mimi, mtumishi wako, nitakuwa na amani"

1 Samuel 20:8

Sentensi Unganishi

Daudi anaendelea kuongea na Yonathani.

na mtumishi wako ... nimemleta mtumishi wako

Daudi anajiambia mwenyewe katika mtu wa tatu kama aina ya unyenyekevu. "Na mimi, mtumishi wako ... amenileta, mtumishi wako "au" pamoja nami ... amenifanya"

umemweka mtumishi katika agano la BWANA pamoja na wewe

Ni nini ambacho wanaume wawili walikubaliana juu yao wanaweza kufanywa wazi. AT 'Yahweh alisikia wakati ulifanya makubaliano mazuri na mimi kwamba wewe na mimi tutakuwa marafiki mara zote'

maana kwa nini basi unipeleke kwa baba yako?

Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "basi hapakuwa na sababu ya kunileta kwa baba yako"

La hasha!

Huu ni msemo ambao una maana kwamba haitafanyika kamwe kwako. AT "Hii haitafanyika kamwe kwako!"

siwezi kukuambia?

Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Mimi hakika nitakuambia."

1 Samuel 20:12

Tazama

"kuangalia" au "kusikiliza" au "kuwa makini kwa kile ninachokuambia"

ikiwa kuna mapenzi mema

"kama baba yangu anataka kufanya mambo mema kwa ajili yenu"

je, nisikutumie taarifa na kulidhihirisha kwako?

Yonathani anatumia swali hili kusisitiza kwamba atamwambia Daudi ikiwa Sauli anataka kumdhuru. Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "basi nitalituma kwenu na kukujulisha"

Bwana atamfanyie Yonathani na zaidi

Huu ndio idiom. Jonathan hutumia kiapo hiki kwa kusisitiza na anajishughulisha mwenyewe kama alikuwa mtu mwingine. AT "Bwana atanifanyia chochote kilichomdhuru baba yangu ananakusudia kukufanyia, na hata zaidi ya hayo"

1 Samuel 20:14

Taarifa za jumla

Yonathani anamwomba Daudi asiwauwe kabisa watoto wake wote ili mabaki yasalie.

hautanionesha uaminifu wa agano la BWANA, kwamba siwezi kufa?

Yonathani anauliza swali hili kuthibitisha kwamba Daudi atafanya jambo hili. Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Tafadhali unionyeshe uaminifu wa agano la Bwana, ili nisipate kufa"

nionesha uaminifu wa agano la Bwana

"Nionyeshe aina ya uaminifu wa agano kwamba Bwana anaonyesha"

nyumba ya Daudi

Neno "nyumba" ni metonym kwa watu wanaoishi ndani ya nyumba. AT "familia ya Daudi"

Bwana awe na uhasimu kutoka kwa mkono wa maadui wa Daudi

Mkono ni kingo kwa mtu. Maana iwezekanavyo ni 1) "Na Bwana awatumie maadui wa Daudi kumuadhabu ikiwa Daudi atavunja ahadi hii" au 2) "Na Bwana awaangamize maadui wa Daudi."

1 Samuel 20:17

alimpenda kama alivyopenda roho yake mwenyewe

Hapa "roho yake mwenyewe" anajielezea mwenyewe. AT "Yonathani alimpenda Daudi kama alivyojipenda mwenyewe"

Hautakuwapo

Hii inaweza kuelezwa katika fomu harisi. AT "Baba yangu atakukosa"

wakati shughuli ikifanyika

Hapa "shughuli ikifanyika" ni idiom ambayo inahusu wakati kila kitu kilichotokea. AT "wakati kila kitu kilichotokea"

jiwe la Ezeli

"Ezeli" ilikuwa jina la jiwe. AT "jiwe ambalo watu huita Ezeli"

1 Samuel 20:20

Sentensi Unganishi

Yonathani anaendelea kusema na Daudi.

kwa upande wake

Hapa neno "wake" linamaanisha jiwe ambalo Daudi alikuwa amejificha.

kijana wangu ... kijana mdogo

Hizi zinarejea mtu huyo huyo.

Tazama

"Sikiliza" au "Kuwa makini na kile nitakachokuambia"

ndipo uje

"ndipo wewe, Daudi, uje"

1 Samuel 20:22

Sentensi Unganishi

Yonathai anaendelea kusema na Daudi.

Tazama

Neno "tazama" hapa linaongeza mkazo kwa kifuatavyo. AT "kweli"

Bwana yupo kati yangu na wewe

Maana iwezekanavyo ni 1) "Bwana ni shahidi kati yako na mimi' au "Bwana ataangalia jinsi tunavyogusa" au 2) "Na Bwana awe shahidi kati yako na mimi" au "Je! Bwana angalia jinsi tunavyohusika kila mmoja nyingine" '^^

1 Samuel 20:24

Yonathani alisimama wima

Nakala za zamani zimekuwa na "Yonathani ameketi karibu naye" (UDB).

1 Samuel 20:26

Hayuko safi; hakika hayuko safi

Kwa mujibu wa sheria ya Musa, mtu asiye najisi kwa sherehe sio kushiriki katika sikukuu mpaka kuhani atangaza kwamba yeye ni safi. Sauli anarudia maneno haya kama anajaribu kujihakikishia.

1 Samuel 20:28

aliniomba ruhusa aende

"aliniuliza nitamruhusu aende"

kama nimepata kibali machoni pako

Hapa macho yanawakilisha kuona, na kuona inawakilisha mawazo au hukumu. kama ilivyotafsiriwa katika 20:3. AT "Nimekufurahia wewe" au "unaniona vizuri"

meza ya mfalme

Yonathani anamzungumzia Sauli kama kwamba yeye ni mtu mwingine kuonyesha kwamba anamheshimu Sauli. AT "meza yako"

1 Samuel 20:30

Hasira ya Sauli iliwaka yakuteketezwa dhidi ya Yonathani

Hapa "hasira ya kuteketezwa" ni metonymy ambayo inamaanisha kuwa hasira sana. AT "Sauli alimkasirika sana Yonathani"

Wee mwana wa mwanamke mkaidi na muasi!

Huu ndio mfano. Sauli anatumia maneno haya kama adhabu kali kwa Yonathani na wasiwasi wake kwa Daudi. AT "Wewe mwana mjinga wa kahaba" au "Wewe mjinga mjinga"

Wadhani kwamba sijui kuwa umemchagua Mwana wa Yese ......chi wa mama

Sauli anatumia swali hili kusisitiza kwamba anajua kwamba Yonathani na Daudi ni marafiki. Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Najua kwamba umemchagua mwana wa Yese ... uchi wa mama."

aibu ya uchi wa mama yako

Hapa "uchi wa mama" ni msemo ambao unamhusu mama aliyekuzaa. AT "kwa aibu ya mama yako aliyekuzaa"

siyo wewe wala ufalme wako utakaoimarika

Hii inaweza kuelezwa katika fomu harisi. AT "huwezi kuwa mfalme na hautaanzisha ufalme wako"

1 Samuel 20:32

Kwa sababu gani inampasa kuuwawa? Amefanya nini?

Jonathan anajaribu kumtia Sauli kufikiria kwa makini kuhusu kile anachofanya. Hii inaweza kutafsiriwa kama taarifa, na maneno "anapaswa kuuawa" yanaweza kutafsiriwa kwa fomu harisi. AT "Huna sababu nzuri ya kumwua. Hakufanya chochote kibaya." au "huna sababu ya kumwua. Hakufanya chochote kibaya."

siku ya pili ya mwezi

Hii "pili" ni namba ya upeo ambayo inahusu mbili. AT "siku ya pili ya tamasha mwezi"

alimhuzunikia Daudi

Hii inaweza kuelezwa katika fomu harisi. AT "alikuwa akimhuzunikia Daudi"

alikuwa amemwaibisha

Hapa "yeye" anaelezea Daudi.

1 Samuel 20:35

kijana alikuwa pamoja naye

Hapa "yeye" ina maana ya Yonathani.

alipiga mshale zaidi yake

"Yonathani alipiga mshale zaidi ya kijana"

mshale hauko mbele yako?

Yonathani hutumia swali hili kusisitiza kwamba mshale ni mbele zaidi ya huyo kijana. Matumizi ya kutafsiri pia inasisitiza hili. Swali la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Unapaswa kujua kwamba mshale ni zaidi ya wewe" au "Mshale ni mbali na wewe"

1 Samuel 20:38

akamwita yule kijana, "Upesi,

"alimwita kijana huyo, ambaye alikuwa akikimbia kutoka kwake," Upesi"

1 Samuel 20:41

kilima

Inaonekana kwamba Daudi alikuwa akificha nyuma ya rundo la ardhi au mawe (tazama UDB).

akiwa amelala kifudifudi, akainama mara tatu

Daudi akainama mbele ya Yonathani, ambaye alikuwa bado mwana wa Mfalme, anastahili heshima hiyo. Pia, hii ndiyo mara ya mwisho Daudi alikutana na Yonathani.

Bwana awe awe kati yako na mimi

Maana iwezekanavyo ni 1) "Yahweh ni shahidi kati ya yako na mimi" au "Yahweh ataangalia jinsi tunavyogusa' au 2) "Na Bwana awe shahidi kati yako na mimi" au "Je! Bwana angalia jinsi tunavyohusika kila mmoja nyingine. Tafsiri kama ilivyo katika 20:22.

1 Samuel 21

1 Samuel 21:1

Nobu

jina la mahari

Ahimeleki

jina la mtu

kutetemeka

kutetemeka kwa hofu

kwa jambo

"kufanya kazi kwa ajili yake"

Nimewaelekeza vijana kwenda sehemu fulani

"Nimewaambia vijana hao kwenda mahali pengine, nami nitakutana nao hapo baadaye" (Angalia UDB)

1 Samuel 21:3

Sasa basi

Daudi anaanza sehemu mpya ya mazungumzo.

chakula gani kinapatikana hapa?

Hapa "kwa upande" ni metonymy ambayo ina maana inapatikana. AT "Ni chakula gani ambacho unaweza kunipa?"

Nipatie mikate mitano

Hili ni ombi la heshima.

mkate wa kawaida

mkate ambao makuhani hawakutumia katika ibada

mkate mtakatifu

mkate ambao makuhani wametumia katika ibada

kama vijana hawajatembea na wanawake.

Hii inaweza kutafsiriwa kama hukumu kamili. AT "Wanaume wako wanaweza kula kama hawajalala na wanawake hivi karibuni"

1 Samuel 21:5

wanawake wamewekwa kutoka kwetu

Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu. AT "tumejiweka wenyewe kwa wanawake"

siku tatu

3 siku

nilipo ondoka

mimi nilipoanza safari

miili ya vijana iliwekwa wakfu

Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu ya kazi. AT "Wanaume waliweka vile ambavyo vimetengwa"

Je, si zaidi sana leo miili yao ikawekwa wakfu

Hii ni kauli, sio swali. Inaweza kutafsiriwa kwa fomu ya kazi. AT "Ni kweli hasa leo kwamba wataweka wakfu vile walivyo navyo"

mkate ambao uliwekwa wakfu

Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu ya kazi. AT "mkate ambao makuhani walikuwa wameweka"

kilicho ondolewa mbele za Bwana, ili waweke

Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu ya kazi. AT "ambayo makuhani waliondoa mbele ya Bwana ili waweze kuweka"

1 Samuel 21:7

Doegi.......wachungaji

Unaweza kuhitaji kusema wazi kwamba Doegi aliona kile Daudi alichofanya. AT " Doegi ... wachungaji, na aliona kile Ahimeleki alivyofanya"

Doegi

jina la mwanaume

ameshilkiliwa mbele za Bwana

Maana iwezekanavyo ni 1) "kwa kuwa Bwana amemzuia hapo," labda Doeg aliweza kumaliza kufanya kitu alichoahidi Bwana angekifanya (angalia UDB) au 2) hakuna mtu anayejua kwa nini alikuwa huko, "kwa sababu fulani"

wachungaji

watunzaji na walinzi wa kundi, hasa ng'ombe au kondoo

1 Samuel 21:8

Sasa hakuna hata mkuki wowote au upanga?

Hapa "upande" ni maana ya metonymy "inapatikana." AT "Je, una mkuki au upanga ambao unaweza kunipatia?" Tafsiri kama katika 21 3.

silaha

jina la jumla kwa mambo kama vile mapanga, visu, upinde na mishale, na mikuki

Bonde la Ela

Hii ndio jina la mahali pa Israeli

1 Samuel 21:10

huyu siye Daudi mfalme wa nchi hii

Walikuwa wakifanya kiburi wakati wakisema Daudi alikuwa mfalme wa nchi hiyo. Walitumia swali hili kuthibitisha kuwa Daudi alikuwa adui mwenye nguvu na Akishi hawapaswi kumruhusu awe kukaa huko. AT "Unajua kwamba hii ni Daudi, ambaye ni hatari kama mfalme wa nchi"

Je hawakupokezana kuimba na kucheza, 'Sauli ..... maelfu

Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Unajua kwamba wakati watu wa nchi walipokuwa wanacheza, waliimba kwa kila mmoja juu yake,' Sauli ... maelfu."

1 Samuel 21:12

Daudi akayaweka maneno hayo moyoni

Hapa "ilichukua ... moyoni" ni hali ya kufikiri kwa bidii juu ya kile kilichosemwa. AT "Daudi alifikiria kwa undani kuhusu yale waliyosema watumishi"

mokononi mwake

Hapa "mikono" ni metonym kwa mtu. "mbele yao"

1 Samuel 21:14

Kwa nini mumemleta kwangu?

Maana iwezekanavyo ni 1) Achish anadai kwamba watumishi wake wanasema kwa nini walimletea Daudi au 2) Akishi anawafukuza kwa swali la uwazi. AT "Unapaswa kujua kuwa hakumletea."

Kwa nini mmemleta kwangu? Je, mimi nina haja na wehu, kumbe mmemleta mtu huyu ili anifanyie hayo mbele yangu?

Swali hili la uhuishaji ni kukataa. AT "Kuna vichaa wa kutosha hapa ambao hupoteza muda wangu. Unapaswa kumleta mtu huyu awe kama mmoja mbele yangu."

Hivi kweli huyu ataingia nyumbani mwangu?

Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Usiruhusu mtu huyu aingie nyumbani mwangu."

1 Samuel 22

1 Samuel 22:1

pango

nafasi ya mashimo chini ya ardhi, kwa ujumla kufungua upande wa kilima, kubwa ya kutosha kwa watu kuingia

Adulamu

Hii ni jina la mji karibu na mji wa Gaza.

waliposikia hayo

aliposikia kwamba Daudi alikuwa amekwenda kujificha katika pango

Kila mmoja aliyekuwa na mahangaiko......kila mmoja ambaye hakuwa na furaha

Hiki ni kisichozidi. AT "Watu wengi ambao walikuwa na shida ... watu wengi ambao hawakuwa na furaha"

jemedari

afisa wa kijeshi anayeongoza askari

mia nne

"400"

1 Samuel 22:3

Kisha Daudi alitoka huko

"Ndipo Daudi akaondoka pango la Adula"

Mispa

Hii ni jina la mji.

nenda pamoja nawe

Daudi alitaka wazazi wake wapate kuishi na mfalme wa Moabu ili Mfalme Sauli asiweze kuwadhuru. Watafsiri wanaweza kueleza maana yake ya msingi kwa kutumia mawazo ya "kuja kukaa na wewe," "kukaa na wewe," au "kuishi hapa na wewe," kama katika UDB.

nenda katika nchi ya Yuda

"nenda kwenye nyumba yako ya Yuda"

Harethi

Hii ni jina la mji.

1 Samuel 22:6

Daudi amepatikana, akiwa pamoja na watu aliokuwa nao

Sauli alikuwa na hamu zaidi kwa Daudi, kwa hivyo mwandishi huwaambia watu wengine tofauti. Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu ya kazi. AT "mtu alikuwa amegundua ambapo Daudi na wanaume wote waliokuwa pamoja naye walikuwa wameficha"

mti wa mkwaju

Hii ni aina ya mti. AT "mti mkubwa wa kivuli"

huko Rama

Rama ni jina la mahali huko Gibea. Jina linamaanisha "mahali pa juu." Inawezekana maana ni 1) inaelezea hapa mahali panaitwa Ramah, au 2) inahusu sehemu yoyote ya juu. AT "kwenye kilima" (UDB)

1 Samuel 22:7

Je, mwana wa Yese atawapa mashamba na mashamba ya mizabibu?

Sauli anatumia swali ili kusisitiza kwamba Daudi, ambaye ni wa kabila la Yuda, hataki kufanya hivyo kwa watu wa kabila la Benyamini. AT "Mwana wa Yese hatakupa mashamba au mizabibu."

Je, mwana wa Yese atawapa

Wakati atakapotoa inaweza kufanywa wazi. AT "Wakati mwana wa Yese atakapokuwa mfalme, atatoa"

mwana wa Yese

"Daudi"

Je, atawafanya nyote kuwa majemedari.... mimi?

Sauli anatumia swali ili kusisitiza kwamba Daudi, ambaye ni wa kabila la Yuda, hataki kufanya hivyo kwa watu wa kabila la Benyamini. AT "Yeye hawezi kukufanya jemedari ... dhidi yangu."

Je, atawafanya nyote kuwa majemedari

Unaweza kuhitaji kutoa wazi wakati atawafanya kuwa maakida. AT "Atakapokuwa mfalme, je, atawafanya ninyi nyota majemedari"

majamedari

maofisa wa kijeshi ambao huongoza askari

1 Samuel 22:9

Doegi Mwedomu

jina la mtu. Tafsiri kama katika 21:7.

Nobu..... Ahimeleki

jina la mahali na jina la mwanadamu. Tafsiri kama katika 21:1.

Ahitubu

jina la mtu

Alimwomba BWANA ili apate kumsaidia, na alimpatia

Ahitubu akamwomba Bwana, ili Bwana amsaidie Daudi, na Ahitubu akampa Daudi

1 Samuel 22:11

kwa kumpatia

"kwa kutoa"

kuinuka

"waasi" au "kupambana"

1 Samuel 22:14

Nani miongoni mwa watumishi wako wote aliyemwaminifu kama Daudi.... nyumbani?

Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Hakuna hata mmoja wa watumishi wako ni mwaminifu kama Daudi ... nyumba."

mlinzi

mtu au kundi la watu wanaolinda mtu

mwenye heshima nyumbani mwako

Neno "nyumba" ni kielelezo kwa familia inayoishi ndani ya nyumba. Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu ya kazi. AT "ambaye familia yako inaheshimu"

Je, leo ni mara ya kwanza kwangu kumuomba Mungu apate kumsaidia?

Ahimeleki anajiuliza swali hili kabla Sauli hajaweza kuuliza, basi mara moja hujibu. Swali hili la uhuishaji linaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Hii sio mara ya kwanza nimeomba kwa Mungu kumsaidia Daudi."

Iwe mbali nami!

msamiati huu una maana "kabisa"

Usimruhusu mfalme awe na shauri kwa mtumishi wake au kwa nyumba yote ya baba yangu. Kwa maana mtumishi wako hajui chochote

Ahimeleki anaongea mwenyewe katika mtu wa tatu kama "mtumishi." Ahimeleki pia anamwambia Sauli katika mtu wa tatu kama 'mfalme." Ahimeleki anaongea hivi kwa njia ya kumheshimu Sauli. AT "Tafadhali, Mfalme Sauli, usione mimi, mtumishi wako, au mtu yeyote katika nyumba ya baba yangu kuwa na hatia. Kwa maana sijui chochote "

shauri

kuzingatia mtu mwenye hatia

nyumba yote ya baba yangu.

Hapa "nyumba" inawakilisha "familia." AT "kwa familia ya baba yangu yote"

1 Samuel 22:16

nyumba ya baba yako

Neno "nyumba" ni kielelezo kwa familia inayoishi ndani ya nyumba. AT "familia ya baba yako" au "wazao wa baba yako"

mlinzi aliyesimama karibu naye

"askari wamesimama karibu ili kumlinda"

Geuka na uwauwe

Hapa "Geuka" ina maana ya kugeuka au ageuka mbali na mfalme. AT "Nenda na kuua" au "Uua"

mkono wake u juu ya Daudi

Neno "mkono" ni msisitizo kwa kazi iliyofanywa kwa mkono. AT "pia wanamsaidia Daudi"

hawakunyoosha mkono wao kuwaua

Neno "mkono" ni msisitizo kwa kazi iliyofanywa kwa mkono. AT"hakufanya chochote kuua" au "kukataa kuua"

1 Samuel 22:18

Geuka na uwauwe makuhani....akageuka na kuwapiga makuhani

Hapa "Geuka" ina maana ya kugeuka au kugeuka mbali na mfalme. Tafsiri kama katika 22:16. AT "Nenda na kuua makuhani ... akaenda na kushambulia" au "Uua kuhani ... aliwashambulia makuhani"

Doegi Mwedomu akageuka na kuwapiga..... akawauwa....... akawapiga...akawauwa

Maana iwezekanavyo ni 1) Doegi aliwauawa makuhani wote mwenyewe au 2) neno "Doegi" ni synecdoche kwa Doegi na wanaume ambao walikwenda pamoja naye. AT "Doegi na wanaume wake waligeuka na kushambulia ... waliuawa ... walishambulia ... Waliuawa"

watu themanini-watano

watu watano - "85 watu "au "85 makuhani"

Kwa makali ya upanga

"Kwa upanga"

aliishambulia Nobu

Hapa "kushambuliwa" inamaanisha kuuawa. AT "aliwaua watu wengi katika jiji la Nobu"

1 Samuel 22:20

Abiathari

Hili ni jina la mwanaume.

1 Samuel 23

1 Samuel 23:1

Kupura

Kutenganisha ngano au mbegu toka kwenye makapi.

1 Samuel 23:3

Je, si zaidi sana kama tutaenda Keila kupambana na majeshi ya Wafilisti?

"tutakuwa na hofu zaidi kama tukienda Keila kupigana na jeshi la Wafilisti."

1 Samuel 23:5

wakaenda ... kupigana ... Wakahamisha ... kuwapiga ... akawaokoa

Mwandishi anamuelezea sana Daudi hapa japikuwa watu wa Daudi walimsaidia kufanya mambo haya yote.

1 Samuel 23:7

Sauli aliambiwa

Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu. AT "Mtu alimwambia Sauli" au "Walisema Sauli"

aliita

"aitwaye" au "wamekusanyika"

1 Samuel 23:10

Daudi akasema

"Daudi aliuliza" au "Daudi aliomba"

mtumishi wako hakika amesikia....... kama mtumishi wako alivyosikia.....mwambie mtumishi wako

Daudi anaongea kama mtu mwingine aliyeonyesha heshima yake kwa Bwana. AT "Nimesikia hakika ... kama nilivyosikia ... niambie"

watanisalimisha mkononi mwake

Hapa "mkono" inawakilisha nguvu au udhibiti. AT "nipe juu ya Sauli"

kuharibu

"kushindwa kabisa"

1 Samuel 23:12

Daudi akasema

"Daudi aliuliza" au "Daudi aliomba"

watanisalimisha mimi na watu wangu katika mkono wa Sauli

Hapa "mkono" inawakilisha nguvu au udhibiti. AT "nipe mimi na watu wangu juu ya Sauli"

1 Samuel 23:13

mia sita

"600"

Sauli akaambiwa

"mtu alimwambia Sauli" au "walimwambia Sauli"

ametoroka

"amemkimbia"

hakumweka mkononi mwake

"hakumruhusu Sauli awe na nguvu juu ya Daudi" au "hakumruhusu Sauli amkamate Daudi"

1 Samuel 23:15

kuangamiza maisha yake

"kujaribu kumuua"

akamtia moyo amtumainie Mungu

akamuhimiza amuamini Mungu

1 Samuel 23:17

Kwa maana mkono wa baba yangu Sauli hautakupata

"kwa maana baba yangu hatakuwa na nguvu juu yako"

1 Samuel 23:19

Je, Daudi hakujificha kati yetu kwenye ... Yeshimoni?

"Daudi amejificha kati yetu kwenye ... Yeshimoni?

Yeshimoni

Hii ni maana nyingine ya "jangwa"

kumtia katika mkono wa mfalme

"kumleta Daudi kwako ili ufanyie kama uavyotaka"

1 Samuel 23:21

Mbarikiwe na BWANA

Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu. AT "Natumaini kwamba Bwana atakubariki"

mmenihurumia mimi

"umeniambia hii"

Jifunze na ujue

Maneno haya mawili yanamaanisha kitu kimoja na inaweza kutafsiriwa kama neno moja. AT "Fahamu kwa uhakika"

nani ambae amemuona

"nani aliyemuona"

Nimeambiwa

Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu ya kazi. AT "Watu wameniambia" au "Nimesikia"

miongoni mwa elfu zote za Yuda

Huu ndio ukweli. AT "hata ikiwa ninahitaji kumkamata kila mtu katika Yuda" au "kati ya jamaa zote za Yuda"

1 Samuel 23:24

Kisha wakasimama

Waliacha kile walichokuwa wakifanya. Msomaji haipaswi kuamini kwamba walikuwa ameketi au amelala.

Kisha wao

"Basi wazifu"

Zifu

Hili ni jina la mahali. Tafsiri hii kama ilivyo katika 23:13.

Yeshimoni

Hili ni jina la eneo la jangwa karibu na Bahari ya Ufu. Inaweza pia kutafsiriwa kama "Jangwa la Yudea" au "uharibifu." Tafsiri kama katika 23:19.

Daudi akaambiwa habari hiyo

Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu . AT "Mtu fulani alimwambia Daudi kwamba walikuwa wanakuja" au "Daudi alijifunza kwamba walikuwa wanakuja"

Mlima wa miamba

mlima uliofunikwa na miamba mingi au majabari

miongoni mwa maelfu wa Yuda

Huu ndio msemo. AT "hata ikiwa ninahitaji kumfunga kila mtu katika Yuda" au "kati ya jamaa zote za Yuda"

1 Samuel 23:26

njoo harakisha

"njoo haraka"

1 Samuel 23:28

kumfuatia

"kumkimbiza" au "kumfuata ili kumkamata"

Mwamba wa maficho

kumbukumbu au alama ya kutoroka kwa Daudim toka kwa Sauli.

1 Samuel 24

1 Samuel 24:1

Akaambiwa

"mtu akamwambia" au "wakamwambia"

elfu tatu

"3,000"

waliochaguliwa

watu waliochaguliwa kwa sababu ya uwezo wao mkubwa wa kivita

jangwa la Engedi

Engedi ni eneo kavu lililokuwa na maji katika Israeli ya mangharibu.

1 Samuel 24:3

mazizi ya kondoo

"boma la kondoo"

kujisaidia

"kwenda haja"

pango

hili ni shimo la asili lililopo chini ya ardhi na lenye uwazi kwenye upande wa kilima

Kisha Daudi akainuka na kumnyemelea kwa mbele kimya kimya

"Daudi alichukua hatua; alimnyemelea taratibu"

kunyemelea

kwenda taratibu

1 Samuel 24:5

moyo wa Daudi ukamchoma

"Daudi alihuzunika kwa sababu alitenda jambo baya"

Mtiwa mafuta wa Bwana

"mtu ambaye Bwana alimchagua kuwaongoza watu wake"

kunyoosha mkono wangu juu yake

"kumdhuru kwa namna yoyote"

1 Samuel 24:8

Kwa nini unawasikiliza watu ambao wanasema, "Angalia, Daudi anatafuta kukudhuru?

"Hupaswi kuwasikiliza watu wanaosema, 'angalia Daudi anatafuta kukudhuru.?"

1 Samuel 24:10

macho yako yameona

Hapa "macho yako" yanawakilisha Mfalme Sauli. AT "umeona kwa macho yako mwenyewe"

alivyokuweka mkononi mwangu

Neno "mkono" ni msisitizo ya udhibiti. AT "kukuweka ambapo ningeweza kukuua au kuruhusu kuishi"

Baba yangu

Sauli hakuwa baba halisi wa Daudi. Daudi anamwita "baba" kuonyesha kwamba anamheshimu Sauli.

hakuna uovu au uasi katika mkono wangu

Daudi anaongea kama uovu na uasi ni vitu vya kimwili ambavyo angeweza kushikilia mkononi mwake. Hapa "mkono" unawakilisha mtu anayefanya au kufanya kitu fulani. AT "Sikufanya chochote kibaya juu yenu, wala sijui juu yenu"

1 Samuel 24:12

mkono wangu hautakuwa juu yako

"kumdhuru kwa namna yoyote"

wazee

"watu walioishi zamani"

1 Samuel 24:14

Mfalme wa Israeli ametoka kumuandama nani? Unamsaka nani?

Swali hili linaweza kutafsiriwa kama sentensi "acha niwaambia mfalme wa Israeli amekuja kumuandama nani. Acha niwaambie ni nani unayemsaka."

Unasaka mzoga wa mbwa

"Unamsaka mtu ambaye hana nguvu kama mbwa aliyekufa"

Unasaka kiroboto

"Unasaka mtu asiye na umuhimu kama kiroboto"

ukaione na ukaitetee sababu yangu

Yaweza kuwa na maana ya 1) "kufanya yaliyo sawa na kutetea sababu yangu" au 2) "kuona kuwa sababu yangu ipo sawa na kupigana kwa ajili yangu"

toka kwenye mkono wako

"ili usiwe na nguvu juu yangu"

1 Samuel 24:16

Mwanangu Daudi

Sauli anazungumza na Daudi kama vile ni mtoto wake kumuonesha Daudi kuwa anampenda.

alinyanyua sauti yake akalia

"alilia kwa nguvu"

1 Samuel 24:17

umenitendea mema

Sauli anakiri kwamba Daudi alionyesha kwamba aliunga mkono Mfalme Sauli na alikuwa mwaminifu kwake kwa kutomwua.

kwa kuwa hukuniua wakati BWANA aliponiweka katika rehema yako

Sauli anakubali kwamba Daudi alichagua kuonyesha huruma na alionyesha uaminifu wake kwa Mfalme Sauli kama mafuta ya Bwana.

1 Samuel 24:19

Kwa kuwa mtu akimpata adui yake, atamwacha aende zake salama?

"Kama mtu akimpata adui yake hatamuacha aende salma"

9Kwa kuwa mtu akimpata adui yake, atamwacha aende zake salama?

Sauli alipoamini kuwa Daudi alikuwa adui yake na akatambua kuwa japokuwa Daudi atakuwa mfalme, Daudi hatachukua ufalmetoka kwa Sauli bali atasubiria muda wa Bwana wa kuchaguliwa.

ufalme wa Israeli utaimarika

"Bwana ataimarisha ufalme wa Israeli" au "Ufalme wa Israeli utaimarika"

katika mkono wako

"kwa mamlaka yako" au "kupitia kazi utakazozifanya"

1 Samuel 24:21

hutawakatilia mbali uzao wang baada yangu

"hutawaua wana wangu na familia zao." Ilikuwa ya kawaida kwa mfalme mpya ambaye hakuwa na mstari wa familia uliopita ili kuua watoto wote wa mfalme wa zamani ili kuzuia yeyote kati yao kumsababisha kiti cha enzi.

hautaliharibu jina langu katika nyumba ya baba yangu

Ni muhimu kwa kila familia katika Israeli kuwa na uzao kutoka kizazi hadi kizazi kinachoendelea jina la familia na urithi wa nchi. AT "huwezi kuharibu familia yangu na uzao" au "utaruhusu familia yangu kuishi"

Daudi na watu wawke

"Daudi na jeshi lake"

1 Samuel 25

1 Samuel 25:1

Waisraeli wote wakakusanyika pamoja na kumwomboleza

Hii inawezekana kuwa kizazi. Idadi kubwa ya watu wa Israeli walikuwa labda huko, lakini wengine hawakuweza kuhudhuria.

wakakusanyika pamoja

wakakutana pamoja

wakamzika nyumbani kwake huko Rama

Inawezekana maana ni kwamba walimzika Samweli 1) katika mji wake wa Rama au 2) katika ardhi ya familia yake huko Rama lakini si kimwili ndani ya nyumba au 3) nyumbani kwake huko Rama.

Daudi akainuka na akashuka

"Daudi na watu wake wakaondok na wakashuka"

1 Samuel 25:2

Kulikuwa na mtu mmoja huko Maoni, na mali zake zilikuwa huko Karmali. Mtu huyo alikuwa tajiri sana. Alikuwa na kondoo elfu tatu na mbuzi elfu moja. Naye alikuwa akiwakata manyoya kondoo wake huko Karmeli. 3Na mtu huyo aliitwa Nabali, na jina la mke wake aliitwa Abigaili. Mwanamke huyo alikuwa mwenye busara na mzuri kwa sura. Lakini mwanaume alikwa mkaidi na mwovu katika mambo yake. Alikuwa wa uzao wa nyumba ya Kalebu.

Baadhi ya watafsiri wanaweza kuweka mawazo haya tofauti. "Kulikuwa na mtu jina lake Nabali, mzao wa nyumba ya Kalebu, aliyekuwa tajiri sana. Aliishi Maoni lakini mali zake zilikuwa Karmali: Alikuwa na kondoo elfu tatu na mbuzi elfu moja. Mtu huyu alikuwa mkaidi na muovu. Mke wake aliitwa Abigaili. Mwanamke huyu alikuwa na busara na mzuri wa sura. Sasa alikuwa akiwakata manyoya kondoo wake.

Maoni

Hili ni jina la mji.

Karmali

Hili ni jina la mji.

Elfu tatu

"3,000"

elfu moja

"1,000"

akiwakata manyoya kondoo wake

"kuwanyoa sufu kondoo wake"

1 Samuel 25:4

akiwakata manyoya kondoo wake

"kuwanyoa sufu kondoo wake"

mkamsalimie kwa jina langu

"mumsalimie kama ambavyo mimi ningemsalimia nimkiwa pale"

Uishi katika baraka

"ninatamani kuwa uishi katika mafanikio"

Uwe na amani na nyumba yako iwe na amani, na wote ulionao

"ninatamani kuwa amani iwe kwako, kwa nyumba yako na vyote unavyomiliki"

1 Samuel 25:7

unao wakata manyoya

"wakata manyoya wako wanafanya kazi" Daudi alitaka watu wake wamwambie hivi Nabali ili afahamu kuwa kondoo wake wapo salama kwa sababu watu wa Daudi waliwasaidia kuwalinda.

hatukuwafanyia ubaya, na hawakupotelewa kitu chochote

Daudi anaonesha ni kwa namna gani yeye na watu wake waliwalinda watumishi wa Nabali na mifugo yao.

Basi vijana wangu wapate kibali machoni pako

"Basi ukapendezwe na vijana wangu"

kwa mtumishi wako

Daudi anaonesha heshima mbele ya Nabali kwa kuwaita watu wake watumishi wa Nabali.

mwanao Daudi

Daudi anazungumza kama vile ni mtoto wa Nabali ili kuonesha heshima kwa Nabali aliyekuwa mtu mzima.

1 Samuel 25:9

vijana wa Daudi

"jeshi la Daudi"

walimwambia Nabali yote haya kwa niaba ya Daudi

"wakampa Nabali ujumbe wote"

Daudi ni nani? Na ni nani mwana wa Yese?

Nabali alimfahamu Daudi ni nani lakini hakutaka kumsaaidia Daudi. "Huyu Daudi mwana wa Yese mnayemzungumzia ni nani ... simfahamu."

wanaotoroka

"wanaowageuka" au "wanaoasi dhidi ya"

mkate wangu

Hapa "mkate" umetumika kama aina yoyote ya chakula.

watu wanaotoka nisikokujua

"watu nisiofahamu wanatoka wapi" au "watu nisiowafahamu"

1 Samuel 25:12

kilichosemwa

"alichokisema Nabali"

akawaambia watu wake

"akaliambia jeshi lake"

ajifunge upanga wake." Kila mtu akajifunga upanga wake. Daudi naye pia akajifunga upanga wake.

"jiandaeni kwa ajili ya vita" Na kila mtu akajiandaa kwa ajili ya vita. Daudi naye akajiandaa.

mia nne

"400"

mia mbili

"200"

walibaki kulinda mizigo

Walibaki katika kambi yao ili kulinda wavamizi wasije kuiba mali zao.

1 Samuel 25:14

kijana mmojawapo alimwambia Abigaili, mke wa Nabali akasema

"Mmoja wa watumishi wa Nabali aligundua kitu ambacho Daudi na watu wake walipanga kufanya, hivyo akaenda kwa mke wa NAbali Abigaili"

Hatukudhurika

"hakuna mtu aliyetudhuru" au "tulikuwa salama"

na hatukupoteza chochote wakati wote tulipotembea nao

Watu wa Daudi waliwazuia wanyama wa mwituni na watu wengine wasiibe mifugo ya Nabali.

1 Samuel 25:16

Walikuwa ukuta

Watu wa Daudi walikuwa kama ukuta unaozunguka mji ambao unawalinda watu wa mji huo toka kwa adui zao.

ubaya unamvizia bwana wetu

"mtu anapanga kumfanyia mambo maovu bwana wetu"

bwana wetu

Mzungumzaji anazungumza juu ya Daudi kwa kuonesha kuwa anamuheshimu Daudi.

1 Samuel 25:18

mia mbili

"200"

mikate

Boflo ya mkate ni kama keki ya mkate.

waliokwisha andaliwa

"kitu ambacho kimekwisha pikwa" au "tayari kwa mtu kukipika"

vipimo

vipimo

bisi

"bisi iliyopikwa"

vishada vya zabibu

"zabibu nyingi"

1 Samuel 25:20

Daudi na watu wake

Daudi na jeshi lake

kwa kifuniko cha mlima

Maana iwezekanavyo ni 1) kwenye kitanda cha chini cha mto mkondo au 2) ambapo watu walikuwa wameficha.

1 Samuel 25:21

Taarifa ya jumla:

Mwandishi anatupa taarifa kabla hajaendelea na simulizi.

Basi Daudi alikuwa amesema, "Hakika ... wa kwake"

Msomaji anatakiwa aelewe kuwa Daudi alisema maneno haya kabla hajasema "Kila mtu afunge upanga wake" katika 25:12

Basi Daudi

Neno "basi" linaonesha kuwa mwandishi ameacha kuandika kuhusu Abigaili na akaanza kuandika kuhusu Daudi.

na vyote alivyonavyo hakuna kilichopotea

"Bado anacho kila kitu ambacho ni chake"

Mungu na anitendee hivyo mimi

"Mungu awapige adui wa Daudi"

wote wa kwake

"watu wote ambao wako chini yake" au "wale wa familia yake"

1 Samuel 25:23

Sentensi Unganishi

Mwandishi amekamilisha kutoa maelezo ya historia, hivyo anaendelea na hadithi.

akaweka mbele ya Daudi na akainama chini ya ardhi

Abigaili alikuwa akijinyenyekeza na kuonyesha kwamba angeitii Daudi kwa sababu alikuwa kiongozi mwenye nguvu

nisikilize

"sikia"

bwana wangu.... mtumishi wako....maneno ya mtumishi wako

"wewe ... maneno yangu." Abigaili anazungumzia mwenyewe na Daudi kama kwamba ni watu wawili tofauti kuonyesha kwamba anaheshimu Daudi.

1 Samuel 25:25

Taarifa ya jumla

Abigaili anaendelea kumshauri Daudi asilipe kisasi.

Nakusihi bwana wangu usimjali ... mimi mjakazi wako ... vijana wa bwana wangu ... bwana wangu ... bwana wangu

Abigaili anajizungumzia mwenyewe kwa Daudi kama vile ni watu wawili ili kuonesha heshima kwa Daudi.

Lakini mimi ... sikuwaona ... uliowatuma

"Lakini kama ... ningewaona ... uliowatuma, Ningewapa chakula"

kumwaga damu

kuua

kulipiza kisasi kwa mkono wako mwenyewe

"kulipiza kisasi mwenyewe badala ya kumuachia Bwana afanye"

adui zako ... wawe kama Nabali

Abigaili anazungumza kama vile Bwana amekwisha muadhibu Nabali. "Natumaini kuwa Bwana atawaadhibu adui zako ... kama atakavyomuadhibu Nabali"

1 Samuel 25:27

Taarifa ya jumla:

Abigaili anaendelea kumuomba Daudi asikasirike.

zawadi hii

Hata hivyo "zawadi" zilikuwa nyingi.

mtumishi wako ... bwana wangu ... bwana wangu ... kosa la mjakazi wako ... bwana wangu ... bwana wangu

Abigaili anajizungumzia mwenyewe kwa Daudi kama vile ni watu wawili ili kuonesha heshima kwa Daudi.

wapewe vijana

"tafadhali wape vijana"

Hakika Bwana atamfanyia bwana wangu nyumba imara.

"Bwana atahakikisha kuwa wazao wa bwana wangu watatumika kama wafalme.

anapigana vita ya Bwana

"anapigana dhidi ya adui wa Mungu:"

uovu hautaonekana ndani yako

"hakuna mtu atakayekuona ukifanhya uovu wowote" au "hautafanya uovu wowote"

1 Samuel 25:29

kukuandama

"kukimbiza" au "kuwinda"

uhai wa bwana wangu utafungwa katika furushi la walio hai na Bwana Mungu wako

"Bwana Mungu wako atayafunga maisha ya bwana wangu katika furushi la walio hai" au "Bwana Mungu wako atakuweka hai pamoja na walio hai"

Maisha ya Bwana wangu

Abigaili anajizungumzia mwenyewe kwa Daudi kama vile ni watu wawili ili kuonesha heshima kwa Daudi.

atayatupa maisha ya adui zako mbali, kama vile kutoka katika mfuko wa kombeo.

"Atawaua adui zako kwa urahisi kama mtu anayetupa kombeo umbali mrefu"

Kombeo

Ni kipande cha ngozi ya mnyama chenye kamba ndefu kwenye miisho yote ambapo mtu anaweza kuweka jiwe na kulirusha umbali mrefu.

1 Samuel 25:30

Senetensi Unganishi

Abigaili anaendelea kujadiliana na Daudi.

bwana wangu.... bwana wangu.....bwana wangu...mtumishi wako

Abigaili anazungumzia mwenyewe na Daudi kama kwamba ni watu wawili tofauti kuonyesha kwamba anaheshimu Daudi. "wewe ... wewe ... wewe ... mimi"

Hii haitakuwa mzigo mkubwa sana kwako

Abigaili anasema kwamba kama Daudi akichagua kutolipa kisasi atakuwa na dhamiri safi wakati Bwana atomfanya awe mfalme wa Israeli. Hii inaweza kuelezwa kwa fomu nzuri. AT "Utakuwa na furaha daima ulifanya kama ulivyofanya"

Bwana atakapomtendea bwana wangu mema

Hiyo ni, wakati Bwana amemfanya awe mfalme baada ya utawala wa Sauli kuisha.

1 Samuel 25:32

Taarifa ya jumla:

Daudi anakubali ushauri wa Abigaili na zawadi zake.

Bwana ... abarikiwe yeye

Hii inaweza kutafsiriwa kama 1) "Namtukuza Bwana ... yeye" au 2) "watu wote wamtukuze Bwana ... yeye"

Na hekima yako imebarikiwa, nawe umebarikiwa, kwa sababu

"Namshukuru Bwana kwa sababu amekubariki wewe kwa kukupa hekima na kwa sababu"

kumwaga damu

mauaji

kwa mkono wangu mwenyewe

"kwa matendo yangu mwenyewe"

1 Samuel 25:34

Taarifa ya jumla:

Daudi anakubali zawadi za Abigaili na anakubali kufanya kama alivyoshauriwa.

kwa hakika asinge salia hata mtoto mmoja wa kiume kwa Nabali

"Nisingemuachia Nabali hata mtoto mmoja mwamaume"

akavipokea kutoka mkononi mwake

"akakubali zawadi zote ambazo aliletewa"

nimeisikiliza sauti yako

"nimesikiliza ulichoniambia nifanye" au "nitafanya kama ulivyonishauri"

1 Samuel 25:36

kulipopambazuka

alfajiri

moyo wa Nabali ulifurahi ndani yake

Nabali alikuwa na furaha sana

1 Samuel 25:37

Taarifa ya jumla:

Bwana anamuhukumu Nabali

divai ilipokuwa imemtoka Nabali

"Nabali hakuwa amelewa tena hivyo hakuwa na furaha tena"

moyo wake ukafa ndani yake

Nabali alishindwa kusogea kwa sababu aliogopa sana afya yake haikuwa nzuri tena yamkini kwa sababu alipata mshtuko.

1 Samuel 25:39

Taarifa ya jumla:

Daudi anajitoa kumlinda Abigaili kwa kumuoa.

Bwana abarikiwe

(1) "namtukuza Bwana" au 2) "watu wote wamtukuze Bwana"

aliyenichukulia hatua ya shutuma yangu kutoka mkono wa Nabali

"aliyenitetea baada ya Nabali kunidhihaki"

aliyenichukulia hatua ya shutuma yangu

Hii yaweza kuwa na maana ya "amenionesha kuwa nililokuwa nalifanya lilikuwa sahihi kwa Kumuadhibu Nabali aliyenidhihaki"

na kumzuia mtumishi wake asifanye maovu

Daudi anazungumza hivi kuonesha heshima kwa Bwana "alinizuia nisifanye uovu"

Na amemrudishia Nabali tendo la uovu juu ya kichwa chake mwenyewe

"amemfanyia Nabdali jambo ambali Nabali alipanga kunifanyia"

juu ya kichwa chake mwenyewe

"juu yake"

akawatuma wakaongee na Abigaili, ili amchukue awe mke wake

"akawatuma watu waongee na Abigaili na kumwambia kuwa Daudi anataka kumchukua awe mke wake.

1 Samuel 25:41

aliinuka, akainamisha uso

Abigaili aliitikia kwa kuinamisha kichwa. Msomaji anatakiwa afahamu kuwa alikuwa amekwisha simama wanaume wale walipokuwa wakiongea naye.

Tazama, mjakazi wako ni mtumwa aoshaye miguu ya watumishi wa bwana wangu

Abigaili anazungumza hivi kuonesha heshima. "tazama mimi nitakutumikia, mtumishi wa bwana wangu Daudi, kwa kuosha miguu yako"

Akaharakisha na kuamka

Haraka alifanya alichopaswa kufanya kwa ajili ya kujiandaa na safari kisha akaamka.

watumishi wake watano waliofuatana naye

Abigaili alikuwa amepanda kwenye punda lakini watumishi wake walitembea

1 Samuel 25:43

Daudi pia alimchukua Ahinoamu ... Sauli alikuwa amempa Palti

Matukio haya yalitokea kabla Daudi hajamuoa Abigaili.

Palti ... Palti

Haya ni majina ya wanaume.

Mikali

Hili ni jina la mwanamke

Galimu

Huu ni mji uliopo kaskazini mwa Yerusalemu.

1 Samuel 26

1 Samuel 26:1

Je, Daudi hakujificha ... jangwa?

"Daudi amejificha ... jangwa!"

mbele ya jangwa

"ambapo unaweza kuliona jangwa"

jangwa

Maana nyingine ni nyika.

Sauli akaamka na kwenda

Sauli akachukua hatua; akaenda"

elfu tatu

"3,000"

watu waliochaguliwa

watu waliochaguliwa kwa sababu ya uwezo wao katika vita"

1 Samuel 26:3

mbele ya jangwa

"ambapo unaweza kuliona jangwa"

jangwa

Maana nyingine ni nyika.

1 Samuel 26:5

Daudi akaamka na kwenda

"Daudi alichukua hatua; akaenda"

Abneri ... Neri

Haya ni majina ya wanaume.

1 Samuel 26:6

Ahimeleki ... Abishai

Haya ni majina ya wanaume.

Seruya

Jina la mwanamke.

nitashuka ... mpaka

Inaonekana kuwa Daudi na watu wake walikuwa kilimani.

Mimi nitashuka

"nitaka kuwa mmoja ambaye nitashuka"

Mungu amemweka adui yako mkononi mwako

"Mungu amekupa kumtawala kabisa adui yako"

nimchome mkuki nimtoboe hadi chini kwa mkuki

"kumuua kwa mkuki"

Sitampiga mara mbili

"sihitaji kkumpiga mara ya mbili"

1 Samuel 26:9

awezaye kunyoosha mkono wake dhidi ya mtiwa mafuta wa BWANA na asiwe na hatia?

"Hakuna awezaye kumpiga mpakwa mafuta wa BWANA na asiwe na hatia"

Kama Bwana aishivyo

"kama kweli Bwana aishivyo"

siku ya kufa kwake itakuja

"atakufa kifo cha kawaida"

1 Samuel 26:11

ninyooshe mkono wangu dhidi ya

"kufanya chochote kumdhuru"

tuondoke

Daudi anamjumuisha Abishai.

sababu usingizi mzito kutoka kwa Bwana uliwaangukia

Bwana alisababisha walele usingizi mzito.

1 Samuel 26:13

Hujibu neno, Abneri?

"Nijibu, Abineri!"

kelele

"kuongea kwa nguvu"

1 Samuel 26:15

Wewe siye mtu jasiri?

"wewe ni mtu jasiri"

Ni nani yuko kama wewe katika Israeli?

Swali hili laweza kutafsiriwa kama sentensi likiwa na maana ya 1) Daudi anaendelea kumkemea Abineri "wewe ni mtu mkuu katika Israeli" au 2) Daudi anaendelea kumwambia Abineri "unataka watu wote wafikiri kuwa wewe ni mtu mkuu sana katika Israeli, lakini siyo."

hukumlinda ... mfalme?

Swali hili linaweza kutafsiriwa kama sentensi. Yaweza kuwa na maan ya 1) Daudi anataka Abneri ajibu au 2) "ulipaswa kumlinda ... mfalme."

1 Samuel 26:17

Mwanangu

Sauli hakuwa baba yake na Daudi. Sauli anazungumza kama vile alikuwa baba yake na Daudi kuonesha kuwa anataka Daudi amuamini na amtii kama vile Daudi anavyomuamini na kumtii baba yake.

Kwa nini bwana wangu anamwandama mtumishi wake?

"bwana wangu hana sababu yoyote ya kumwandama mtumishi wake"

Nimefanya nini?

Yaweza kuwa na maana ya 1) Daudi anataka Sauli amjibu swali hili au 2) "unajua kabisa sijafanya lolote kukudhuru."

Mkononi mwangu kuna uovu gani?

Yaweza kuwa na maana ya 1) "unajua kuwa sijafanya lolote bata kwako" au 2) "unaona kuwa sijapanga kukufanyia lolote baya"

1 Samuel 26:19

nakusihi, bwana wangu mfalme asikilize maneno ya mtumishi wake ... mfalme wa Israeli

"wewe mfalme wangu, sikiliza maneno yangu ... wewe"

amekuchochea dhidi yangu

"kusababisha wewe uwe na hasira juu yangu"

aikubali sadaka

"nitampa sadaka ili asisababishe tena uwe na hasira juu yangu"

Walaaniwe mbele za Bwana

"Bwana aamue kuwaadhibu"

maana leo wamenifukuza, nisishikamane na urithi wa Bwana; wameniambia, 'Nenda ukaabudu miungu mingine.'

"kwa maana leo wamenifukuza. Kwa sababu wanataka nisishikamane na urithi wa Bwana. Wameniambia 'nenda ukaabudu miungu mingine'"

usiiachilie damu yangu ianguke ardhini

"usiniue"

kiroboto mmoja

Daudi alitumia neno "kiroboto" kuonesha kuwa mtu au yeye mwenyewe hawezi kufanya madhara makubwa. "mimi sitakudhuru tena kama kiroboto mmoja awezavyo"

nisishikamane na urithi wa Bwana

"kwamba nisiamini tena kuwa Bwana atanipa mimi alichoniahidi"

kama vile mtu awindavyo kware milimani

Sauli alimkimbiza Daudi kama vile anawinda mnyama wa maana wa mwituni.

1 Samuel 26:21

Rudi

Yaweza kuwa na maana ya 1) "rudi unitumikie katika mahali pangu" au "rudi nyumbani kwako"

Mwanangu

Sauli hakuwa baba yake na Daudi. Sauli anazungumza kama vile alikuwa baba yake na Daudi kuonesha kuwa anataka Daudi amuamini na amtii kama vile Daudi anavyomuamini na kumtii baba yake.

maisha yangu yalikuwa yenye thamani machoni pak

"umeonesha kuwa unaniheshimu kabisa"

nimetenda upumbavu

"nimekuwa mpumbavu"

1 Samuel 26:22

Bwana likuweka mkononi mwangu

"Bwana alinipa nafasi ya kukuvamia leo"

amlipe

"heshima" au "tuzo"

mtiwa mafuta wake

"aliyechaguliwa kuwa mfalme"

1 Samuel 26:24

maisha yako yalikuwa ya thamani machoni mwangu

"nimekuonesha kuwa ninakuheshimu"

hivyo maisha yangu yathaminiwe sana machoni pa Bwana

"na Bwana ayathamini maisha yangu kama vile nilivyoyathamini maisha yako"

Na ubarikiwe

"Na Bwana akubariki"

mwanangu

Sauli hakuwa baba yake na Daudi. Sauli anazungumza kama vile alikuwa baba yake na Daudi kuonesha kuwa anataka Daudi amuamini na amtii kama vile Daudi anavyomuamini na kumtii baba yake.

1 Samuel 27

1 Samuel 27:1

Daudi alisema moyoni mwake

"Daudi alifikiri mwenyewe"

nitaponyoka kutoka mkono wake

"nitamtoroka yeye"

1 Samuel 27:2

Daudi akaondoka na kuvuka

"Daudi alichukua hatua; akavuka"

kuvuka

"akavuka mpaka kati ya Israeli na Philistia"

Watu mia sita

"600"

Sauli akaambiwa

"mtu alimwambia Sauli" au "Sauli alisikia"

1 Samuel 27:5

Kama nimepata kibali machoni pako

"kama nimekupendeza" au "kama utanitendea wema"

wanipatie mahali

"tafadhali nipatie mahali"

mojawapo ya miji ya nchi

"mojawapo ya miji nje ya jiji"

kwa nini mtumishi wako akae pamoja na wewe katika mji wa kifalme?

"Mimi sio wa muhimu sana mpaka nikae pamoja na wewe katika mji wa kifalme"

Mtumishi wako

Daudi anazungumza kwa kuonesha heshima kwa Akishi.

1 Samuel 27:8

wakiteka nyara

Mara nyingi walivamia na kuchukua mali.

Wagirizi

Kundi la watu waliokuwa wakiishi kati ya Filistia na Misri.

uelekeo wa kwenda Shuri

"njiani ambapo watu wengi walisafiri kuelekea Shuri"

Shuri

Ni mkoa uliokuwepo kaskazini mwa mpaka wa Misri.

Akishi

Mfalme wa Gathi.

1 Samuel 27:10

Akishi

Mfalme wa Gathi.

Wayerameeli,

Ukoo toka kabila la Yuda.

Wakeni

Kundi la watu lililoishi katika nchi ya Midiani.

1 Samuel 27:11

Gathi

Moja ya miji mikuu mitano ya Wafilisti.

Akishi

Mfalme wa Gathi.

1 Samuel 28

1 Samuel 28:1

jeshi

Kundi kubwa la majeshi.

Daudi akamwambia Akishi, "Sasa ... kufanya." Akishi akamwambia Daudi, "Basi ... mlinzi."

Neno "basi" linaonesha kuwa mzungumzaji amekubaliana na mtu mwingine kwa aliyoyasema. "Daudi alimwambia Akishi kuwa, 'kwa sababu umesema hivyo, ... fanya.' Akishi akawambia Daudi, 'kwa sababu umefanya hivyi, ... mlinzi.'"

utajua kile ambacho mtumishi wako anaweza kufanya

Daudi alitaka Akishi afikiri kuwa Daudi atawaua Wafilisti wengi, lakini "mtumishi wako anaweza kufanya" inamaana kuwa Daudi alipanga kuwaua Wafilisti.

Mtumishi wako

Daudi anazungumza kwa kuonesha heshima kwa Akishi.

Nitakufanya

Hapa anazungumziwa Daudi.

mlinzi

"mtu anayemlinda mtu mwingine"

1 Samuel 28:3

Sasa Samweli ... na pepo

Mwandishi anaonesha mwanzo wa simulizi ili kumuandaa msomaji kwa ajili ya matukio yanayofuata.

amewafukuza kutoka nchini

Kuondolewa rasmi toka kwenye nchi au mji au kuzuiwa kuingia.

wale walioongea na wafu au pepo

Maneno haya "wale walioongea na wafu" yatafsiri kwa neno moja kwa lugha asili na maneno "wale walioongea na pepo" pia tafsiri neno moja kwa lugha ya asili. Kama lugha yako ina neno moja lenye maana ya wale wanaoongea na pepo au wale wanaoongea na wafu unaweza kutumia maneno haya hapa.

Wafilisti walijikusanya

Baada ya Daudi na Akishi kuzungumza.

akawakusanya Israeli wote pamoja,

"akakusanya jeshi lake lote katika Israeli pamoja"

Shunemu ... Gilboa

Haya ni majina ya mahali.

1 Samuel 28:5

aliogopa na moyo wake ukatetemeka sana

Maneno haya yana maana sawa na yanasisitiza hofu aliyokuwa nayo.

Urimu

Kuhani mkuu alibeba kura takatifu inayoitwa Urimu na Thumimu katika ngao yake.

kuongea na wafu

Maneno haya yatafsiri kwa neno moja la lugha ya asili. Kama lugha yako ina nono moja kwa mtu anayezungumza na wafu unaweza kutumia neno hilo hapa.

Endori

Hili ni jina la mahali.

1 Samuel 28:8

Sauli akajigeuza ... akaondoka... yule mwanamke wakati wa usiku

Sauli alijigeuza kwa sababu njia ya kutoka Giboa kwenda Endori ilikuwa ya kupitia mahali ambapo Wafilisti waliishi. Alisafiri siku nzima na kumfikia mwanamke baada ya jua kuzama.

Kujigeuza

Kubadilisha mwonekano wake wa kawaida ili mtu yeyote asimtambue.

wale wanaoongea na wafu au mizimu

Maneno haya "wale walioongea na wafu" yatafsiri kwa neno moja kwa lugha asili na maneno "wale walioongea na mizimu" pia tafsiri neno moja kwa lugha ya asili. Kama lugha yako ina neno moja lenye maana ya wale wanaoongea na mizimu au wale wanaoongea na wafu unaweza kutumia maneno haya hapa.

Nitabirie ... na wafu

"ongea na waliokufa kwa niaba yangu"

Maisha yangu

Neno "maisha" inasimama badala ya mtu.

1 Samuel 28:13

mungu

Yaweza kuwa na maana ya 1)"Hakuna kama Mungu" au 2) "hakimu"

1 Samuel 28:16

amerarua ufalme kutoka mkononi mwako

"amemfanya mtu mwingine kuwa mfalme katika nafasi yako"

1 Samuel 28:18

BWANA atamweka Israeli pamoja na wewe katika mkono wa Wafilisti

"Bwana atawaruhusu Wafilisti wawafanyie chochote wanachotaka kuwafanyia wewe pamoja na watu wa Israeli"

mtakuwa pamoja nami

Hii ni njia nzuri ya kumwambia Sauli kuwa atakufa.

BWANA pia ataliweka jeshi la Israeli katika mkono wa Wafilisti

"Bwana atawaruhusu Wafilisti wawafanyie chochote wanachotaka kuwafanyia jeshi la Israeli"

1 Samuel 28:20

kwa kuwa siku hiyo alikuwa hajala chakula, hata kwa usiku huo wote

Sauli hakula chakula usiku kabla ya safari kutoka Gilboa mpaka Endori, wala mchana wakati wa safari wala usiku alipokwenda kumtembelea mwanamke.

Nimeyaweka maisha yangu mkononi mwangu na nimeyasikiliza

"Ninaweza kufa kwa sababu nimesikiliza"

1 Samuel 28:22

sauti ya mjakazi wako mwanamke

Mwanamke anazungumza kwa namna hii kuonesha kuwa anamuheshimu Sauli.

alikataa

"hakukubali" au "hakufanya kama walivyomuomba"

wakamlazimisha

"wakamuhimiza"

1 Samuel 28:24

ndama mnono

Ndama ambaye amekua na amelishwa kuwa tayari kwa ajili ya sikukuu maalumu.

yeye ... akaukanda

Alichanganya unga na mafuta, akachanganya ma mikono yake ili kutengeneza unga kwa ajili ya kuoka.

1 Samuel 29

1 Samuel 29:1

chemchemi

Ni mkondo mdogo wa maji unaotoa maji toka ardhini.

wakapita na mamia kwa maelfu

"akaenda pamoja na kundi la mamia kwa kundi la maelfu"

mamia ... maelfu

100 ...1,000

Daudi na watu wake wakapita wakiwa wa mwisho pamoja na Akishi

Kundi la watu mamia na ma walipita kwanza kisha Akishi na wasaidizi wake na Daudi, watu wake na askari wengine wa Wafilisti waliokuwa wakimlinda Akishi.

1 Samuel 29:3

Hawa Waebrania wanafanya nini hapa?

Yaweza kuwa na maana ya 1) "hukupaswa kuwaruhusu Waebrania hawa, adui zetu kuwa hapa pamoja na sisi." au 2) "Tuambie Waebrania hawa ni akina nani."

Huyu si Daudi ... kwa miaka hii ... hadi leo

Hii ina maana ya "Unatakiwa kufahamu kuwa huyu ni Daudi ... miaka hii. Nimeona ... siku hii.."

nami nimeona hana kosa

"Sijui lolote baya alilolifanya" au "Nimependezwa naye sana"

1 Samuel 29:4

usimruhusu aende nasi vitani

"usirihusu jeshi lake liungane na jeshi letu dhidi ya adui zetu"

Kwa jinsi gani mtu huyu angeweza kufanya amani na bwana wake? Siyo kwa gharama ya vichwa vya watu wetu?

"Njia pekee ya Daudi kufanya amani na Bwana wake ni kwa kuua askari wetu!"

1 Samuel 29:5

Je, huyu siye Daudi ambaye walimuimba kwa kupokezana na kucheza, wakisema, 'Sauli ... makumi elfu'?

Hii yaweza kutafsiriwa kama "hupaswi kumuamini Daudi - yeye ndiye wanayemuimba kwa kupokezana na kucheza, wakisema 'Sauli ... makumi elfu'!

elfu ... makumi elfu

"1,000 ... 10,000"

1 Samuel 29:6

Kama Bwana aishivyo

"Hii ni kauli ya kweli"

kutoka kwako na kuingia kwako pamoja nami katika jeshi ni kwema

"Nina furaha kwa sababu umetoka na kuingia pamoja nami na jeshi langu"

1 Samuel 29:8

bwana wangu mfalme

Daudi anazungumza na Akishi ili Akishi afikiri kuwa Daudi anamuheshimu. "wewe, bwana wangu na mfalme"

hata hivyo, wale wakuu

"hatahivyo, wakuu"

1 Samuel 29:10

bwana wako

Msomaji anatakiwa aelewe kuwa Akishi anamzungumzia Sauli.

kupata mwanga

"unaweza kuona kwa kutumia jua la asubuhi"

1 Samuel 30

1 Samuel 30:1

Ziklagi

Huu ni mji uliopo kusini mwa Yuda. Huku ndiko ambapo Daudi na watu wake waliziweka familia zao.

Wao

Waamaleki

Mkubwa na mdogo

Yaweza kuwa na maana ya 1) "watu wasio na umuhimu na wenye umuhimu" au 2) "watu wakubwa na wadogo"

1 Samuel 30:3

wake zao ... watoto wa kiume ... na watoto wa kike

Waliokuwa wanamuhusu Daudi na watu wake

umechomwa moto, na wake zao... binti zao walichukuliwa mateka

"waliwaona watu wakichoma moto na kuchukua wake zao ... mateka"

watu aliokuwa nao

Hawa walikuwa watu wa jeshi lake.

1 Samuel 30:5

Taarifa ya jumla:

Daudi anapata nguvu kwa Bwana baada ya uvamizi.

Ahinoamu Myezreeli

"Ahinoamu toka Yezreeli"

Nabali Mkarmeli

"Nabali toka Karmeli"

Ahinoamu ... Abigaili

Haya ni majina ya wanawake

dhiki

Mateso

roho za watu wote zilihuzunika

"watu wote walikuwa tayari kuasi dhidi ya Daudi" au "watu wote hawakuwa na furaha"

Daudi alijiimarisha katika BWANA, Mungu wake

Yaweza kuwa na maana ya 1) "Daudi alijiimarisha kwa sababu alijua kuwa Bwana Mungu wake atamsaidia" au 2) "Bwana Mungu wake alimpa nguvu Daudi"

1 Samuel 30:7

Taarifa ya jumla:

Daudi anaomba maelikezo toka kwa Bwana juu ya wavamizi wa watu wake.

Daudi akamwomba BWANA kwa ajili ya mwongozo

"Daudi alimuomba Bwana ili amwambie ni nini anapaswa kufanya"

nikiliandama

"kufukuza" au "kufuata"

1 Samuel 30:9

watu mia sita

"600"

kijito

mto mdogo

kuandama

"kufukuza" au "kufuata"

watu mia nne

"watu 400"

mia mbili

"watu 200"

waliokuwa wamechoka

Hawakuwa na nguvu tena ya kuendelea.

1 Samuel 30:11

Mmisri shambani

Aliachwa hapo ili afe na kundi la Waamaleki wavamizi.

vishada vya zabibu

"vishada vya zabibu zilizokauka"

1 Samuel 30:13

Daudi akamuuliza

Daudi akamuuliza swali mtumwa wa Misri.

siku tatu zilizopita

"siku tatu kabla"

mashambulizi

uvamizi katika mji na kuchukua mali.

1 Samuel 30:15

jeshi lililofanya mashabulizi

ni kundi la mashujaa wenye silaha wanaovamia watu au mahali ghafla.

hautaniua ... kunisaliti na kuniweka katika mikono ya bwana wangu

"hautaniua ... kuvunja uaminifu nilionao kwako kwa kumruhusu bwana wangu anitawale tena.

1 Samuel 30:16

nyara

mali zilizoibiwa katika uvamizi

jua lilipozama

muda baada ya jua kuzama mpaka anga linapokuwa na giza.

mia nne

"400"

1 Samuel 30:18

akawaokoa

"aliwaokoa" au "kuwa huru"

Hakuna kilichopotea

"hakuna kilichopotea kati ya vilivyochukuliwa na Waamaleki"

si kidogo wala kikubwa

Yaweza kuwa na maana ya 1) "watu wasio na umuhimu na wenye umuhimu" au 2) "watu wakubwa na wadogo"

nyara

mali zilizoibiwa na Waamaleki.

1 Samuel 30:21

mia mbili

"200"

kijito

mto mdogo

Besori

Hili ni jina la mto mdogo.

kumlaki

"kumkaribisha"

nyara

mali zilizochukuliwa toka kwa adui katika vita.

kurudisha

"kupata tena"

1 Samuel 30:23

Ni nani atawasikiliza kuhusu jambo hili?

"Hakuna atakayewasikiliza katika jambo hili"

Kwa maana mgawo ni kwa yeyote aendae

"kwa maana ni kwa ajili ya kila mtu aendaye"

yeyote aendae vitani

mashujaa waliopigana katika vita

watapata tena kilicho sawa

"atahakikisha kuwa kila mtu anapokea kiasi sawa"

yeyote aliyelinda mizigo

watu waliowasaidia mashujaa kutunza na kilinda vitu vyao

mzigo

vitu ambavyo mashujaa waliviacha nyuma walipokwenda vitani

1 Samuel 30:26

Taarifa ya jumla:

Mwandishi anaandika miji ambayo wazee wake walipokea zawadi toka kwa Daudi.

Ziklagi ... Bethueli ... Yatiri ... Aroeri ... Sifmothi ... Eshtemoa

Haya ni majina ya miji.

nyara

vitu ambavyo Daudi alivichukua toka kwa Waamaleki baada ya vita.

zawadi

hedaya

1 Samuel 30:29

Taarifa ya jumla:

Mwandishi anamalizia majina ya miji ambayo wazee wake walipewa zawadi na Daudi.

Rakali ... Horma ... Borashani ... Athaki

Haya ni majina ya miji.

Wayerameeli ... Wakeni

Haya ni majina ya makundi ya watu.

1 Samuel 31

1 Samuel 31:1

Basi Wafilisti wakapigana dhidi ya Waisraeli.

Vita hivi ni matokeo ya ugonvi kati ya Daudi na wafilisti katika sura ya 29:10.

Wafilisti wakapigana dhidi ya Waisraeli

"Wafilisti wakapigana dhidi ya watu wa Israeli"

mlima wa Gilboa

Hili ni jina la mlima.

wakamwandama Sauli na wanawe kwa karibu

"walimfukuza Sauli na watoto wake watatu"

Abinadabu, and Malkishua

Haya ni majina ya wanaume.

Vita vikamwelemea Sauli

"jeshi la Sauli likaanza kushindwa katika vita"

1 Samuel 31:4

mbeba silaha

Mbeba silaha alibeba ngao kubwa ya jemadari wake na silaha zingine.

hawa wasiotahiriwa

"watu hawa ambao hawajatahiriwa" au "watu ambao sio Waisraeli"

hakukubali

"hakukubali kufanya kile ambacho Sauli alimwambia afanye"

alichukua upanga wake mwenyewe na kuuangukia

"akajiua mwenyewe kwa upanga wake"

siku iyo hiyo

"siku hiyo moja"

1 Samuel 31:7

kukaa humo

kushi kwenye miji ambayo watu wa Israeli waliondoka

nyara za waliokufa

kuchukua silaha katika miili ya Waisraeli waliokufa.

Mlima Gilboa

Mlima unaoelekea bonde la Yezreeli kaskazini mwa Israeli toka Nazareti.

1 Samuel 31:9

pande zote katika nchi ya Wafilisti

"maeneo yote katika nchi ya Wafilisti"

kutangaza habari

"kuwaambia watu"

mahekalu yao ya sanamu

majengo ambayo waliabudu sanamu zao

Ashtorethi

huyu ni mungu wa uongo na sanamu

kutundika

"kubandika" (yaweza kuwa kwa kutumia msumari)

Bethi Shani

Hili ni jina la mji.

1 Samuel 31:11

Yabeshi

Hili ni jina la mji.

kile ambacho Wafilisti walimfanyia Sauli

"namna ambavyo Wafilisti walimdharau Sauli"

usiku wote

"usiku kucha"

Mkwaju

Huu ni aina ya mti, "mti mkubwa wenye kivuli"

2 Samuel 1

2 Samuel 1:1

Siku ya tatu

"Baada ya siku tatu"

Nguo zake zikiwazimeraruliwa na akiwa na vumbi juu ya kichwa chake

Katika utamaduni huu, mtu kurarua mavazi yake na kuweka vumbi kichwani pa mtu lilikuwa tendo la kuombolezo.

Aliinamisha uso wake chini na kujifanya yeye mwenyewe kuwa si kitu

Hili lilikuwa ni tendo la kuonesha utii kwa Daudi, ambaye kwa wakati huo alikuwa mfalme wa Israeli.

2 Samuel 1:3

Wengi wameanguka na wengi wameuawa

Maana yake yaweza kuwa 1) "Wengi walikuwa wamejeruhiwa na wengine walikuwa wameuawa" au 2) "Wengi walikuwa wamejeruhiwa na kuuawa."

2 Samuel 1:6

Kwa bahati nilikuwa

Taarifa hii inasisitiza kwamba mtu yule hakuwa amepanga kukutana na Sauli

Sauli alikuwa ameegemea mkuki wake

Maana yake yaweza kuwa 1) Sauli alikuwa amedhoofika na alitumia mkuki kumsaidia au 2) Sauli alikuwa akijaribu kujiuwa kwa kuuangukia mkuki wake.

2 Samuel 1:8

Akaniuliza, 'Wewe ni nani?' Nikamjibu, 'Mimi ni Mwamaleki.'

Nukuu hii ingeweza kutaarifiwa kama kauli tendwa. Mfano "Aliniuliza mimi nilikuwa nani, nami nikamwambia kuwa nilikuwa Mwamaleki"

Mimi ni Mwamaleki

Hawa ni watu walewale Daudi aliokuwa ametoka kuwashambulia katika 1:1.

shida kubwa imenipata

Shida ya Sauli inasemwa kama kitu cha kutisha ambachokimemshikilia. Maana nyingine yaweza kuwa "nimeteswa vibaya sana"

uhai ungalimo ndani yangu

Nahau hii inamaanisha kwamba yu ngali hai au "ningali hai"

asingeweza kuishi baada ya kuwa ameanguka

"Hata hivyo angekufa tu"

2 Samuel 1:11

Daudi akararua mavazi yake... watu waliokuwa pamoja naye wakafanya vilevile

Daudi na watu wake walirarua mavazi yao kama ishara ya kuomboleza kwa ajili ya Mfalme Sauli.

alikuwa ameanguka

Hii inamaanisha "alikuwa ameuawa."

Kwa upanga

Hapa upanga unahusianishwa na vita, yaweza kumaanisha "katika magwanda ya kijeshi"

Unatoka wapi?

Yule mtu alikuwa amekwisha eleza kuwa yeye ni Mwamaleki katika 1:8. Bila shaka Daudi anamwuliza yule mtu kuthibitisha kwa sababu ya hukumu kali aliyokuwa anaelekea kuitamka juu ya mtu yule.

2 Samuel 1:14

Kwa nini hakuogopa kumwua mtiwa mafuta wa Yahwe... mkono?

Mbalaga ni swali linalotumika kumkemea mtu. inaweza kutafsiriwa kama taarifa. Ulipaswa kumwogopa Yahwe na usingemwua mtiwa mafuta wake... mkono!"

Mfalme aliyetiwa mafuta na Yahwe

Usemi huu unasimama badala ya Sauli, ambaye alikuwa amechaguliwa na Mungu.

mkono wako

Kirai hiki kinaonesha kufanya jambo fulani wewe mwenyewe, wewe "mwenyewe" au "binafsi"

Mpige chini

Nahau hii inamaanisha "alimwua."

Damu yako i juu ya kichwa chako

Hapa "damu" inaonesha "kumwaga damu" na inahusishwa na kifo. Hapa "kichwa chako" inamwonesha yule mtu na inamaanisha kwamba anawajibika. Yaani "unahusika kwa kifo chako mwenyewe" au "Umesababisha kifo chako mwenyewe"

kinywa chako kimeshuhudia dhidi yako

Hapa "kinywa chako mwenyewe" inamwone yule mtu mwenyewe. "Umejishuhudia mwenyewe"

2 Samuel 1:17

Maelezo kwa Ujumla

Daudi anaimba wimbo wa maombolezo kwa Sauli na Yonathani

Wimbo wa Upinde

Hili lilikuwa jina la wimbo

Kitabu cha Yashari

Neno "Yashari" humaanisha "Unyofu."

iliyoandikwa katika Kitabu cha Yashari

Hii ni taarifa ya mwanzo iliyoongezwa kumweleza msomaji yaliyotendeka katika wimbo

Utukufu wako, Israeli, umekufa

"Utukufu wako" inamwonesha Sauli.

Wenye uwezo

Kifungu "wenye uwezo" inamhusu Sauli na Yonathani. Kisifa nomino hiki kipo katika wingi, na kinaweza kutaarifiwa kama "wenye uwezo"

wameanguka

Neno "wameanguka" linamaanisha "kufa"

Msisema katika Gathi...msiitangaze katika mitaa ya Ashkeloni

Vifungu hivi viwili vinamaanisha jambo moja na vimerudiwa kama sehemu ya ushairi wa wimbo

Gath...Ashkeloni

Gathi na Ashkeloni ni miwili kati ya miji mikubwa ya Wafilisiti. Wafilisiti walimwua Sauli na Yonathani

ili binti za Wafilisiti wasifurahi...ili binti za wasiotahiriwa wasisherehekehee.

Vifungu hivi viwili vinamaanisha jambo moja na vimerudiwa kama sehemu ya ushairi wa wimbo.

binti za wasiotahiriwa

kifungu hiki kinawahusu watu wasiomfuata Yahwe, kama vile Wafilisiti.

2 Samuel 1:21

Milima ya Gilboa

Daudi anaongea moja kwa moja kwa "Milima ya Gilboa" kama kwamba ilikuwa ikisikiliza wimbo wake

Haya na kusiwe na umande juu yenu

Daudi analaani ardhi alipofia Mfalme Sauli vitani. Hii ilikuwa siyo heshima kwa Sauli, aliyekuwa mfalme mtiwa mafuta wa Mungu.

ngao ya mwenye uwezo imechafuliwa

"Mwenye uwezo" hapa inaonesha kwa Sauli. Ngao ilichafuliwa kwa sababu ilianguka juu ya ardhi, na kwa sababu damu ya mfalme ilimwagwa juu yake.

Ngao ya Sauli haijatiwa mafuta tena

Ngao ya Sauli ilikuwa imetengenezwa kwa ngozi. Ili kuitunza, ilipakwa mafuta. Inaweza pia kutafsiriwa kuwa "hakuna mtu atayeijali ngao ya Sauli tena"

Kutoka katika damu yao waliouawa, kutoka miili ya wenye nguvu, upinde wa Yonathani haukurudi nyuma, na upanga wa Sauli haukurudi patupu

Sauli na Yonathani wanaoneshwa hapa kuwa wapiganaji hatari na mashujaa.

upanga wa Sauli haukurudi patupu

Upanga wa Sauli unazungumziwa kama kitu hai kwamba ungeweza kurudi wenyewe. Badala ya kurudi patupu, ulikuwa ukiwa na damu ya adui wa Sauli uliowauwa.

2 Samuel 1:23

hawakutenganishwa wakati wa kufa kwao

Kirai "hawakutenganishwa"kinasisitiza kuwa walikuwa pamoja wakati wote. Inaweza pia kuwa kwamba "hata wakati wa kufa kwao walikuwa pamoja"

Walikuwa wepesi kuliko tai, walikuwa na nguvu kuliko simba.

Sauli na Yonathani wanaongelewa kana kwamba walikuwa na kasi kuliko tai na nguvu kuliko simba.

aliyewavika mavazi ya thamani pamoja na vito vya thamani, na aliyetia mapambo ya dhahabu katika mavazi yenu.

"Aliyewapa mavazi mazuri na mapambo." Virai viwili hivi vinamaana moja inayolenga juu kuwaandalia wanawake mavazi ya thamani na ya kuvutia.

2 Samuel 1:25

Jinsi wenye uwezo walivyoanguka

Kifungu hiki kinajirudia katika mstari wa 25 na 27 kusistiza kwamba mashujaa hodari wa Israeli wamekufa. Inaweza pia kuwa "Watu wenye uwezo wamekufa vitani.

wenye nguvu

"nguvu" hapa ina wingi na inaweza kumhusu Sauli na Yonathani pekee, au askari wote wa Israeli. Inaweza pia kuwa mashujaa wenye nguvu.

wameanguka

hii ni njia laini ya kusema "wamekufa vitani."

Yonathani amekufa

Hii inaweza kutaarifiwa katika kauli tendaji. Yaani "Yonathani amekufa vitani" au adui amemwua Yonathani"

Juu ya mahali pako pa juu

Daudi anaendelea kuielekeza sehemu hii ya wimbo katika milima ya Gilboa kama alivyoanza katika 1:21.

Yonathani ndugu yangu

"ndugu" hapa imetumika katika hali ya urafiki wa karibu sana.

Upendo wako kwangu ulikuwa wa ajabu, kupita upendo wa wanawake.

Hapa "upendo" umetumika katika hali ya urafiki na uaminifu. Uaminifu wa Yonathani kwa Daudi ulikuwa mkuu kuliko uaminifu alionao mwanamke kwa mmewew na watoto.

silaha za vita zimeangamizwa

"silaha zao zimeharibiwa"

2 Samuel 2

2 Samuel 2:1

baada ya haya

Baada ya Daudi kuomboleza kifo vya Sauli na Yonathani vitani.

panda katika mojawapo ya miji ya Yuda

Siklagi ulikuwa chini katika mwinuko kuliko Yuda. Inaweza pia kuwa "uendee mmojawapo ya miji ya Yuda"

Daudi akaenda pamoja na wakezi wawili.

Siklagi ulikuwa chini kuliko Hebroni. Inaweza kuwa pia kwamba "Daudi alisafiri kwenda Hebrani pamoja na wake wake wawili"

2 Samuel 2:4

Daudi alitiwa mafuta kuwa mfalme

Katika tendo hili la fumbo, walitia mafuta juu ya kichwa cha Daudi kuonesha kwamba amechaguliwa kuwa mfalme.

nyumba ya Yuda

Hapa "nyumba" imetumika kuonesha kabila. Yaani kabila la Yuda.

Yabeshi Gileadi

Hili ni jina la mji katika eneo la Gibea.

2 Samuel 2:6

Maelezo kwa Jumla

Daudi anaongea na watu wa Yabeshi Gileadi

Jambo hili

Walimzika Sauli

mikono yenu itiwe nguvu

Hapa "mikono" inawaonesha watu wa Yabeshi Gileadi. Yaani "mwe imara"

wamenitia mafuta kuwa mfalme

Katika tendo hili, walimimina mafuta juu ya kichwa cha Daudi kuonesha kwamba alikuwa amechaguliwa kuwa mfalme.

2 Samuel 2:8

Ner...Ishboshethi

Haya ni majina ya wanaume

Mahanaim...Gileadi...Yezreeli

Haya ni majini ya sehemu

2 Samuel 2:10

nyumba ya Yuda

Hapa ''nyumba" imetumika kumaanisha "kabila"

nyumba ya Yuda ilimfuata Daudi

Kutii utawala wa Daudi kunaoneshwa kama kumfuata. Yaani "kabila la Yuda walimtii Daudi kama mfalme wao"

2 Samuel 2:12

Abneri...Neri...Ishboshethi...Sauli...Seruya

Haya ni majina ya wanaume

2 Samuel 2:14

Abneri

Abneri alikuwa ni binamu wa Mfalme Sauli katika Agano la Kale

-inuka,inuka,inuka,inuka, inuka

-inuka, inuka juu - kwa ujumla, neno "inuka" linamaanisha"inuka juu" au "weka juu."

Benjamini

Alikuwa mtoto mdogo kuliko wote aliyezaliwa kwa Yakobo na mke wake Raheli. Jina linamaanisha, "mwana wa mkono wangu wa kuume"

2 Samuel 2:16

walianguka chini pamoja

Hii ni njia nyepesi ya kusema walikufa. Yaani "walikufa wote wawili"

Helkathi Hazzurimu

Hili ni jina lilitotolewa kuwakumbusha watu kilichotokea pale.

Vita ilikuwa kali sana siku ile

Inaweza kusaidia kueleza kwa ufupi kwamba hii ilikuwa vita kubwa iliyotokea baada ya mashindano ya vijana. Yaani "Wengine pia walianza kupigana pia. Ilikuwa vita kali sana siku hiyo"

2 Samuel 2:18

Seruya...Yoabu...Abishai...Asaheli...Abneri

Haya ni majina ya wanaume

Asaheli alikuwa mwepesi miguuni kama swala.

Hapa Asaheli analinganishwa na swala, mnyama akimbiaye kwa kasi sana.

swala pori

Mnyama huyu mdogo mwenye miguu minne, na pembe mbili ndefu kichwani, hukimbia haraka sana.

Akimfuatia bila kugeuka upande mwingine

Hapa "bila kugeuka" imeelezwa kwa muundo hasi kusistiza ukaribu alioifuata njia ya Abneri.

2 Samuel 2:20

Asaheli

Hili ni jina la mwanaume

Kugeuka...geuka upande

"usinifuate...acha kumfuata Abneri"

kamata mmojawapo ya vijana na uchukue silaha yake

Abneri alikuwa akimwambia Asaheli kuua na kumteka askari kijana ambaye siyo hatari kama Abneri. Hakutaka kumwua Asaheli.

2 Samuel 2:22

Kwa nini nikupige hata chini

Swali hili lisiloitaji jibu linatumika kumwonya Asaheli hatari iliyomkabili. "Kupiga hadi chini" ni njia laini ya kusema "kuuwa." Yaani "sitamani kukuuwa."

Jinsi gani basi ningeweza kumtazama usoni Yoabu, nduguyo?

Swali hili lisilohitaji jibu linasisitiza kwamba Abneri hapendi kupigana na kumwua Asaheli kwa sababu ingeharibu uhusiano wake na Yoabu. Hapa "kuinua uso wangu kwa Yoabu" inamaanisha angekuwa na aibu sana kumtazama Yoabu.

geuka upande

Hii inamaanisha "kuacha kumfuatia"

sehemu ya mwisho ya mkiki wake

Hii inaonesha mpini, ambayo siyo kali au kuweza kuchoma kitu. Inaweza kuwa kwamba Abneri alikuwa akijaribu kumzuia Asaheli asimfuatie, na hakukusudia kumwua.

2 Samuel 2:24

Abishai

Hili ni jina la mwanamme

kilima cha Ama...Gia

Haya ni majina ya sehemu

2 Samuel 2:26

Kuita

"piga kelele"

Ni lazima upanga urarue daima?

Swali hili linasisitiza kwamba vita ilikuwa imeendelea muda mrefu. Hapa "upanga" inaonesha mapigano. Mauaji katika vita yanaoneshwa kama mnyama wa mwituni anakula askari. Inamaanisha pia "Hatuitaji kutumia kupigana na kuuana."

Je haujui kwamba itakuwa uchungu mwishowe?

Swali linatumika kumlazimisha Yoabu kukubari kwamba kuendelea kupigana kungeishia maafa makubwa. Hapa "uchungu" ni neno lililotumika kuonesha matesa makali ambayo yangetukia.

Je hata lini utawazuia watu wako wasiwafuatie ndugu zao.

Swali hili linakusudiwa kumshawishi Yoabu kuacha kupigana na Waisraeli wenzake. Hapa "ndugu" inawakilisha watu wa taifa la Israeli. Yaani "Acha sasa jambo hili ili Waisraeli wasiendelee kuuana.

kama Mungu aishivyo

Hiki ni kiapo kikubwa sana. Inamaana ya "pamoja na Mungu kama shahidi wangu" au "Mungu anathibitisha kuwa namaanisha ninachosema."

kama usingesema hivyo...kuwafuatia ndugu zao hata asubuhi

Taarifa hii ya kukisia inaongelea ambacho kingetokea kama Abneri asingemwambia Yoabu kwa hekima.

2 Samuel 2:28

piga tarumbeta

tarumbeta zilitumika kuashiria agizo kulingana na umbali.

kuwafuatia Israeli tena

Hapa "Israeli"inaonesha watu waliokuwa wanapigana upande wa Israeli.

Araba...Mahanaimu

Haya ni majina ya sehemu

2 Samuel 2:30

Asaheli

Hili ni jina la mwanamme

watu 360 wa Benjamini pamoja na Abneri

"watu 360 kutoka Benjamini waliomfuata Abneri." Abneri hakufa.

wa Benjamini

Kifungu kinamaanisha "kutoka kabila la Benjamini."

Kumwinua Asaheli

"waliochukua mwili wa Asaheli"

Siku ikawia asubuhi huko Hebroni

"walifika Hebrono alfajiri asubuhi iliyofuata."

2 Samuel 3

2 Samuel 3:1

Sasa

Neno limetumika hapa kuonesha mkato katika habari kuu. Samweli hapa anatoa habari kuhusu vita kati ya Daudi na wafuasi wa Sauli.

nyumba

hapa "nyumba" inamaanisha "wafuasi."

kuwa imara zaidi na zaidi

kifungu hiki kinamaana ya idadi ya watu waliomsaidia Daudi kuongezeka

kudhoofika zaidi na zaidi

kifungu hiki kinamaanisha kupungua kwa idadi ya walioisaidia nyumba ya Sauli

2 Samuel 3:2

wana walizaliwa kwa Daudi

Hii inaweza kutaafiwa katika muundo tendaji. Yaani wake wa Daudi walizaa wana sita

mzaliwa wa kwanza...mwana wa pili...tatu

Hii ni hesabu kwa mpangilio wa wana wa Daudi

Ahinoamu...Abigaili...Maaka

Haya ni majina ya wanawake. Ni wake wa Daudi.

Kileabu...Nabali...Talmai

Haya ni majina ya wanaume.

2 Samuel 3:4

mwana wa nne...mwana wa tano...wa sita

Hii ni hesabu ya mpangilio wa wana wa Daudi

Shefatia...Ithreamu

Haya ni majina ya wana wa Daudi

Haggithi...Abitali...Egla

Haya ni majina ya wakeze Daudi.

2 Samuel 3:6

Ikawa

Inatambulisha tukio jipya katika habari ya mzozo kati ya wafuasi wa Daudi na familia ya Sauli.

Nyumba ya Sauli

Inaonesha familia ya Sauli na wafuasi waliochukuo umiliki wa maeneo yake alipokufa.

nyumba ya Daudi

Inaonesha wafuasi wa Daudi.

Abneri akajipa nguvu katika nyumba ya Sauli

Kuongezeka kwa nguvu ya Abneri juu ya familia ya Sauli kunasemwa kama alikuwa na nguvu za mwili. Yaani "Abneri akawa na nguvu zaidi juu ya familia na wafuasi wa Sauli"

Rizpa...Aiya

Haya ni majina ya wanawake.

Ishboshethi

Hili ni jina la kiume, mwana wa Sauli.

Kwa nini ulilala na suria wa baba yangu?

Isboshethi anauliza swali hili kumkemea Abneri akifanya kama mfalme. Yaani "Haukuwa na haki ya kulala na suria wa baba yangu!"

kulala na

Hili ni linalopunguza ukali wa neno likimaanisha kukutana kimwili.

2 Samuel 3:8

Je mimi ni kichwa cha mbwa aliye wa Yuda?

Swali hili limetumiwa na Abnera kama hasira ya kukataa lawama ya Isboshethi. Hinaweza kufasriwa kama taarifa. Yaani "mimi siyo msaliti nikimtumikia Daudi!"

mkonono mwa Daudi

Hapa "mkono"inawakilisha nguvu ya kushinda.

Na bado leo unaniraumu kwa ajili ya huyu mwanamke?

Abneri anauliza swali hili kwa ajili ya kumkemea Ishboshethi. Haiko wazi kama kweli Abneri alilala na Rispa, au kama aliraumiwa kwa uongo. Maana yake inaweza kuwa 1) Abneri alikuwa na hatia. Yaani "haupaswi kujisikia vibaya kwamba nililala na mwanamke huyu!" au 2) Abneri hakuwa na hatia. Yaani "haupaswi kudhani kwamba nimelala na mwanamke huyu!"

2 Samuel 3:9

Mungu na anitendee hivyo ...na zaidi pia, ikiwa sifanyi

Huu ni muundo wa nadhiri ya dhati katika siku hizo. Abneri anamwomba Mungu amhukumu kw a ukali asipoitunza nadhiri yake. Lugh yako mara nyingi ina njia ya kuonesha kiapo. Yaani "namwomba Mungu kuniadhibu nisipotenda.

nyumba ya Sauli

Hapa "nyumba" inaonesha familia na wafuasi wa liosalimiki katika kifo cha Sauli.

kiti cha enzi cha Daudi

Kifungu hiki kinaonesha mamalaka ya Daudi kama mfalme.

2 Samuel 3:12

kwa Daudi

Baadhi ya matoleo yanaongeza "alipokuwa huko Hebroni" na mengine yameondoa hiyo. Unaweza kuongeza kifungu ikiwa kimo katika toleo la taifa.

Nchi hii ni ya nani?

Nakala la halisi ya swali hili haiko wazi. Maana pendekezwa ni 1) Abneri alikuwa na nguvu ya kumpa Daudi nchi. Yaani "Nchi hii ni yangu au 2) Daudi amechanguliwa na Mungu kuitawala nchi: Yaani nchi hii ni haki yako.

mkono wangu uko pamoja nawe

Hapa "mkono" unawakilisha msaada waa Abneri anaoutoa kwa Daudi. Yaani:"Nitakusaidia"

hautauona uso wangu mpaka umlete kwanza Mikali

Daudi anaeleza masharti ya kukutana na Abneri. Hapa "uso" inamhusu Daudi mwenyewe. Yaani: "Hautaniona mpaka umlete Mikali kwanza.

Mikali

Hili ni jina la binti Sauli. Alikuwa mke wa kwanza wa Daudi.

2 Samuel 3:14

magovi mia moja ya Wafilisiti

Hii inawakilisha namba ya watu aliowaua Daudi ili Sauli amruhusu kumwoa Mikali. Govi ni sehemu iliyojikunja inayofunika kiungo cha uzazi cha mwanamme.

kumtoa kwa mme wake

Paltieli alikuwa mme wa pili wa Mikali. Sauli alimpa baada ya Daudi kumkimbia Sauli.

Paltieli... Laishi

Haya ni majina ya wanaume

Bahurimu

Hili ni jina la kijiji.

2 Samuel 3:17

Basi fanya hivyo

"Hivyo sasa mfanyeni Daudi kuwa mfalme wenu"

Kwa mkono wa mtumishi wangu Daudi

Hapa "mkono" unataja nguvu ya Daudi kuwashinda Wafilisiti. Yaani nitamtia nguvu mtumishi wangu Daudi"

mkono wa Wafilisiti

Hapa "mkono" unaonesha nguvu juu ya Israeli. Yaani:"nguvu ya Wafilisiti"

mkono wa adui zao wote

Hapa "mkono" unaonesha nguvu juu ya Israeli. Yaani: "nguvu ya adui zao wote"

2 Samuel 3:19

ishirini kati ya watu wake

Idadi ya watu waliokuja na Abneri

watu wa Benjamini...nyumba yote ya Benjamini

taarifa zote mbili zinahusu wazao wa Benjamini, waliokuwa mojawapo ya makabila ya Israeli

2 Samuel 3:21

Israeli wote

Kifungu himi kinamaanisha "wote katika taifa la Israeli."

Hivyo Daudi akamruhusu Abneri kuondoka

Waliachana kama marafiki. Daudi hakuwa amemkasirikia Abneri.

2 Samuel 3:22

mateka

Hivi ni vitu vinavyochukuliwa kutoka kwa adui.

Abneri hakuwa na Daudi huko Hebroni

Tiyari Abneri alikuwa ameondoka kurudi nyumbani.

wakamwambia Yoabu

"mtu fulani alimwambia Yoabu"

Neri

Hili ni jina la mwanamme. Yeye ni babu wa Sauli.

2 Samuel 3:24

Umefanya nini?

Hili ni swali lililoulizwa na Yoabu ili kumkemea Daudi kwa kumwacha Abneri kuondoka kwa amani. "Usingefanya hivi!"

Kwa nini umemwacha aondoke?

Yoabu anauliza swali hili kwa kumkemea Daudi kwa kumwacha Abneri kutoroka. Inaweta kufasiriwa kama taarifa. Yaani "Abneri alikuwa hapa nawe umemwacha aondoke!"

Je haujui...kila ukifanyacho?

Yoabu anauliza swali hili kumshawishi Daudi kuamini kwamba Abneri anapanga njama dhiki ya Daudi. Yaani: "Hakika unajua... kila ukifanyacho."

Kisima cha Sira

"Sara" ni jina la mahali kisima kilipokuwa.

2 Samuel 3:27

katikati ya lango

Hii inahusu mojawapo ya malango katika ukuta wa mji huko Hebroni. Kama UDB inavyoonesha, malango ya mji yalijengwa kama sehehu ya majengo yaliyowekwa ukutani. Ndani ya njia kulikuwa na milango kuelekea vyumba vya ndani, mahali wageni wangepokelewa na biashara na shughuli za kimahakama zingefanyika. Yawezekana ilikuwa ndani ya mojawapo ya vyumba hivi Yoabu alimwua Abneri

damu ya Asaheli

Hapa "damu"inahusishwa na kifo cha Asaheli. Yaani: "kifo cha Asaheli"

Asaheli

Hili ni jina la mwanamme.

2 Samuel 3:28

Neri...Abishai...Asaheli

Haya ni majina ya wanaume.

damu ya Abneri

"Damu" hapa inahusu kifo cha Abneri.

iwe juu ya kichwa cha Yoabu

Kifungu kinamaanisha tokeo la hatia litakuwa juu ya Yoabu na familia yake kama kitu kizito kilichoanguka juu yao. Yaani kusababisha "matatizo kwa Yoabu siku zote"

nyumba yote ya baba yake

"Nyumba" hapa inahusu vizazi. Kifungu "nyumba yote ya baba yake" kinarejea kwa uzao wote wa baba wa Yoabu.

Kusikosekane kuwa

Huu ukanushi wa kujirudia unasisitiza kuwa kutakuwa na mtu daima mwenye matatiza yaliyoainishwa.

ameuawa kwa upanga

"Upanga" hapa unarejesha kwa kifo kibaya. "Yaani alikufa vibaya"

anayekwenda bila chakula

"mwenye njaa"

2 Samuel 3:31

Rarua mavazi yako, vaa gunia

Haya yalikuwa matendo ya kuonesha uzuni.

Mfalme alilia kwa sauti

Maneno "alilia" na "alilia kwa sauti" kwa kawaida yanamaanisha kitu kimoja na yanasisitiza jinsi gani Daudi alimwombolezea Abneri.

2 Samuel 3:33

Je ilimpasa Abneri kufa kama afavyo mpumbavu?

Hili swali lisiloitaji jibu hutumika kuonesha kwamba kifo chake hakikuwa cha haki.

Mikono yako haikuwa imefungwa. Miguu yako haikuwa imefungwa minyororo.

Sentensi mbili hizi zinaonesha wazo moja. Yanaweza kuunganishwa katika sentense moja. Yaani "Haukuwa mwalifu gerezani" au "ulikuwa mwenye haki kwa kutofanya kosa"

Mikono yako haikuwa imefungwa

Hii inaweza kuelezwa katika kauli tendaji. Yaani "Hakuna aliyekuwa amekufunga mikono"

Miguu yako haikuwa imefungwa

Hii inaweza kuelezwa katika kauli tendaji. Yaani "Hakuna mtu aliyekuwa amekufunga minyororo miguu.

wana wa uovu

Hii inarejea kwa watu wasio haki au waovu.

2 Samuel 3:35

watu wote wakaja

Huku kutia chumvi kwa kukusudia kunatumika kuonesha kuwa taifa la Israeli kumjari Daudi katika uzuni yake. Yaani:"Watu wengi walikuja"

Mungu na anifanyie hivyo, na zaidi, ikiwa

Huu ni muundo wa nadhiri ya dhati wakati huo. Daudi anamwomba Mungu kumhukumu kwa ukali ikiwa atakula chochote kabla ya jua kuchwa. Yaani "Ninamwomba Mungu anaifanyie hivyo ikiwa"

2 Samuel 3:37

Je hamjui kwamba mtu mkuu ameanguka leo hii katika Israeli?

Swali hili lisilodai jibu limetumika kuonesha jinsi Daudi alivyomweshimu Abneri. Hapa "kuanguka"ni neno linalomaanisha "kifo". Inaweza kutafsiriwa kama taarifa. Yaani: Ni wazi kwamba mtu mkuu amekufa leo katika Israeli!"

mwana mfalme na mtu mkuu

Vifungu hivi viwili vyote vinamrejerea Abneri.

Neri...Seruya

Haya ni majina ya wanaume.

ukatili

"bila huruma"

2 Samuel 4

2 Samuel 4:1

Ishbosheth...Baana...Rekabu...Rimoni

Haya ni majina ya wanaume.

Basi mwana wa Sauli alikuwa na watu wawili...muda huu

Hii inawatambulisha Baana na Rekabu katika habari.

mikono yake ikadhoofika

Katika kifungu hiki "mikono yake" inamwakilisha Ishboshethi. Yaani: "Ishboshethi akadhoofika au kupoteza nguvu"

maana Beerothi pia ilihesabiwa kuwa sehemu ya Benjamini, na Wabeerothi walikimbilia Tittaim na wamekuwa wakiishi pale mpaka sasa

Hapa mwandishi anatoa mazingira ya Beerothi kwa msomaji. Beerothi ilikuwa sehemu ya nchi ya Benjamini.

Beeroth...Gittaim

Haya ni majina ya sehemu.

2 Samuel 4:4

Maelezo kwa Jumla

Mstari huu unaacha habari kuu na kutoa maelezo ya mazingira kuhusu Mefiboshethi, uzao wa Sauli kupitia Yonathani badala ya Ishboshethi. Baadaye Mefibosheshi atakuwa mhusika mhimu katika kitabu.

Umri wa miaka mitano

Huu ulikuwa ni umri wa mwana wa Yonathani wakati wa kifo cha baba yake.

Kilema cha miguu

Kifungu kinamaanisha "kutokuweza kutembea."

habari kuhusu Sauli na Yonathani

Hii inarejea kwa taarifa kuhusu vifo vyao.

Mlezi

Huyu ni mwanamke au msichana aliyeajiriwa kulea watoto wadogo

akawa kilema

Hii inaeleza jinsi Mefiboshethi alivyojeruhiwa hivyo kutokuweza kutembea.

Mefiboshethi

Hili ni jina la mwana wa Yonathani, mjukuu wa Sauli.

2 Samuel 4:5

Maelezo kwa Jumla

Habari inarudi kwa tendo la Baana na Rehabu waliokuwa wemetambulishwa katika 4:1

Joto la mchana

Mchana, sehemu ya siku ambapo joto ni kali zaidi

kupepeta ngano

"kuondoa makapi kutoka katika ngano.

2 Samuel 4:8

anatafuta maisha yako

usemi unamaanisha "anataka kukuua."

Kama aishivyo Yahwe

Hii ni kati ya nadhiri zenye nguvu Daudi alizoziapa, kama ambavyo Yahwe ni shahidi. Yaani: "Naapa kwa uhai wa Yahwe"

aliyeniuokoa uhai wangu

"Uhai" hapa unarejea kwa Daudi mwenyewe. Yaani "aliyeniokoa"

2 Samuel 4:11

Ni kiasi gani zaidi...nisiutake uhai wake kutoka mkononi mwako, na kukuondoa kutoka duniani?

Swali hili linaonesha kwamba watu walikuwa wametenda kosa kubwa sana. Inaweza kutafsiriwa kama taarifa. Yaani: "hata unahatia kubwa zaidi! Ni wajibu wangu kutaka damu yake kutoka mkononi mwako na kukuondoa duniani."

kutaka damu yake mkononi mwako

Kifungu "damu yake" kinawakilisha uhai wa Ishboshethi. Hapa "kutoka mkononi mwako"inawakilisha Rehab na Baana, wana wa Rimon Mbeerothi kutoka 4:5. Yaani: "tazama unawajibika kwa kifo cha Ishboshethi"

kata mikono na miguu yao na kuwatundika

Hii yalikuwa matendo ya kuonesha ukali kwa hao watu.

wakakichukua kichwa cha Ishboshethi na kukizika kaburini

hili lilikuwa ni tendo la kuonesha heshima kwa Ishboshethi. Hii ingeweza kuelezwa kwa ufupi. Yaani "walimweshimu Ishboshethi kwa kuzika kichwa chake kaburini."

2 Samuel 5

2 Samuel 5:1

tu nyama na mfupa wako

Kifungu kinamaanisha "undugu." Yaani "sisi tunauhusiano nawe" au sisi tu wa familia moja."

wakati mfupi uliopita

Hii ni habari ya kihistoria. Sauli alikuwa mfalme wao kabla ya Daudi.

Utawachunga watu wangu Israeli, nawe utakuwa mtawala juu ya Israeli

Vishazi viwili hivi vinamaanisha kimsingi jambo moja na linasistiza kwamba Yahwe alikuwa amemchagua Daudi kuwa mfalme.

Utawachunga watu wngu Israeli

Hapa kuwatawala watu kunazungumzwa kana kwamba ni kuwachunga. Yaani: "utawaangalia watu wangu Israeli" au "Utatawala juu ya Israeli watu wangu"

2 Samuel 5:3

Wakamtia mafuta Daudi kuwa mfalme juu ya Israeli

"Kutiwa mafuta" ni tendo la alama ya kuonesha kwamba wanatambua kwamba Mungu alikuwa amemchagua Daudi kama mfalme.

2 Samuel 5:6

Maelezo kwa Jumla

Daudi na jeshi la Israeli wanaishambulia Yerusalemu

Hautaingia humu isipokuwa utazuiwa na vilema na vipofu

Hii inaweza kuelezwa katika muundo chanya. Yaani: "ikiwa utakuja hapa, hata vipofu na vilema wataweza kukuondoa."

vipofu na vilema

Watu wasioweza kuona wala kutembea

2 Samuel 5:8

Daudi akasema, "Watakaowapiga Wayebusi

Daudi alikuwa akiongea na askari wake. Yaani: Daudi aliwambia askari wake, "Wanaotaka kuwa ondoa Wayebus" (UDB)

'Vipofu na vilema'

Maana pendekezwa ni 1) hii inarejerea kwa watu ambao ni vilema na vipofu kweli au 2) hii ni maana inayoonesha Wayebusi ndani ya Yerusalemu kama wote walikuwa dhaifu na wasio na uwezo.

2 Samuel 5:11

Hiram

Hili ni jina la mwanamme

mafundi selemala

wanaoshughulika na mbao

Wajenzi

wanaojenga

2 Samuel 5:13

Shamua...Shobabu...Nathani...Sulemani...Ibari...Elisha...Nefegi...Eliada...Elifeleti

Haya ni Majin ya wana wa Daudi

wana na binti walizaliwa kwake

hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji. Yaani: "alikuwa na wana zaidi na mabinti" au "walimzalia wana zaidi na mabinti"

waliozaliwa kwake

Hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji. Yaani "kwamba wakeze walimzalia" au "alikuwa"

2 Samuel 5:17

Daudi alikuwa ametiwa mafuta kama mfalme juu ya Israeli

Hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji. Yaani: "Israeli walikuwa wamemtia mafuta Daudi kama mfalme"

wakatoka wate wakimtafuta

Kifungu hiki kinarejea kwa baadhi ya Wafilisiti wakimtafuta Daudi.. Kina tia chumvi kuonesha ni kiasi gani Wafilisiti walivyotaka kumpata Daudi.

Bonde la Mrefai

Hili ni jina la mahali

2 Samuel 5:19

Baali Perazimu

Hili ni jina la sehemu.

Yahwe amewafurikia adui zangu mbele zangu kama mafuriko ya maji

Daudi anazungumzia ushindi aliompa Yahwe kama yalikuwa mafuriko yaliyopitiliza kingo zake na kuifunika nchi, yakisababisha uharibifu. Yaani: "Yahwe amewashinda adui zangu kama mafuriko yanavyoishinda nchi"

2 Samuel 5:22

Wafilisiti wakaja tena

"Walikuja" kwa sababu Wafilisiti waliishi upande wa chini kuliko ngome ya Daudi.

Bonde la Mrefai

Hili ni jina la sehemu.

miti ya miforosadi

"Miforosadi" ni aina ya miti, na "miti" inaelezea miti ya miforosadi iliyopamoja.

2 Samuel 5:24

Mtakaposikia...Yahwe atakuwa amekwenda mbele yenu kulipiga jeshi la Wafilisiti

Hii ni mwendelezo wa maelekezo ya Yahwe kwa Daudi yaliyoanza katika 5:22. Yahwe hapa anajisema katika nafsi ya tatu.

Mtakaposikia sauti ya kwenda katika upepo ukivuma kupitia juu ya miti ya miforsadi

"Wakati upepo unavuma kupitia juu ya miti ya miforsadi kama watu wanaotembea"

Geba...Gezeri

Haya ni majina ya mahali.

2 Samuel 6

2 Samuel 6:1

Basi

Neno hili linaonesha sehemu mpya ya taarifa.

watu wote wateule wa Israeli

Aina hii ya maana inawakilisha jeshi la taifa la Israeli.

Elfu thelathini

"30,000"

kutoka Baala katika Yuda kulileta sanduku kutoka pale

Inaonesha kuwa wanalichukua sanduku kutoka Yerusalemu. Yaani: "kutoka Baala uliopo Yuda kulipeleka Sanduku la Mungu huko Yerusalemu"

kulileta sanduku la Mungu kutoka pale

Yerusalemu ilikuwa juu kuliko pengine sehemu nyingine yoyote katika Israeli, hivyo ilikuwa kawaida kwa Waisraeli kusema kukwea au kushuka kutoka Yerusalemu.

kulipandisha

Neno "leta" laweza kutafsiriwa kama "chukua."

Baala

Hili ni jina la mahali

ambalo linaitwa kwa jina langu Yahwe wa majeshi

Jina la Yahwe lilikuwa limeandikwa juu ya sanduku.

akaaye juu ya makerubi

"akaaye katika sehemu ya mamlaka kati ya makerubi"

kukaa katika kiti cha enzi

kukaa juu ya kiti cha enzi au mahali pa mamlaka

2 Samuel 6:3

Maelezo kwa Jumla

Daudi na jeshi la taifa la Israeli wanaliondoa sanduku la agano.

Abinadabu...Uza...Ahio

Haya ni majina ya wanaume.

nyumba yote ya Israeli

Aina hii ya maana inawakilisha watu wa Israeli. Yaani: "Waisraeli wengine wote pamoja nao"

Matari

Hiki ni chombo cha kimziki kama kichwa cha ngoma pamoja na vipande vya chuma kuzunguka sehemu inayosikika kifaa kinapotikiswa au kupigwa.

kayamba

chombo cha mziki chenye vitu vingi vidogo vigumu ndani yake, ikifa sauti ya kimziki kinapotikiswa

Matowazi

Sahani mbili nyembamba za chuma zinazogongwa pamoja kufanya sauti ya juu.

2 Samuel 6:6

Nikoni

Hili ni jina la mwanaume.

hasira ya Yahwe ikawaka

Hapa "hasira ya Yahwe" inaongelewa kama ilikuwa ni moto.

kwa dhambi zake

Ilikuwa ni dhambi ya Uza kulishika sanduku kwa sababu Yahwe alikuwa ameamru kwamba kusiwepo mtu atakayeligusa sanduku.

2 Samuel 6:8

Peresi Uza

Hili ni jina la mahali. Mtu anayetafasiri anaweza kuongeza maelezo ya chini kusema, "Jina Peresi Uza linamaanisha 'adhabu ya Uza."'

hadi siku hiyo

Hii inamaanisha hadi wakati habari hii ilipokuwa inaandikwa, siyo sasa katika karne ya ishirini na moja.

Jinsi gani sanduku la Yahwe lije kwangu?

Daudi anatumia swali hili kusisitiza kwamba anaogopa kulipeleka sanduku Yerusalem. Yaani: "Ninaogopa sana kulileta sanduku la Yahwe Yerusalemu."

2 Samuel 6:10

Obedi Edomu Mgiti

Hili ni jina la mwanamme.

alimbariki

"Yey" hapa inarejerea kwa Obedi Edomu Mgiti.

2 Samuel 6:12

Basi

Neno hili linaanza kama sehemu mpya ya habari.

Daudi aliambiwa

Hii inaweza kutaarifiwa katika muundo tendaji. Yaani: "watu walimwambia mfalme Daudi"

Nyumba ya Obedi Edomu

"Nyumba" hapa inawakilisha familia. Yaani: "Obedi Edomu na familia yake"

wakalileta sanduku la Mungu

Yerusalemu ilikuwa juu kuliko karibu eneo lolote katika Israeli, hivyo ilikuwa kawaida kwa Waisraeli kuzungumzia kupanda kwenda au kushuka kutoka Yerusalemu. Yaani: "kuondoa sanduku la Mungu"

kupandisha

Neno "kuleta" laweza kufasiriwa kuwa "chukua."

2 Samuel 6:14

Daudi akacheza mbele ya Yahwe kwa nguvu zake zote

Kucheza hapa ni aina ya kumwabudu Yahwe kwa furaha.

kitani

nguo iliyotengenezwa kutokana na nyuzi za mti wa kitani.

nyumba yote ya Israeli

Hapa "nyumba" inawakilisha watu wa Israeli. Yaani: "Waisraeli wengine wote pamoja naye"

kulipandisha sanduku la Yahwe

Yerusalemu ilikuwa juu pengine kuliko eneo lolote katika Israeli, hivyo ilikuwa kawaida kwa Waisreali kusema juu ya kupanda kwenda au kushuka kutoka Yerusalemu.

kupandisha

kifungu hiki"kupandisha" chaweza kufasiriwa kama "chukua."

2 Samuel 6:16

Basi...moyoni mwake

Neno "basi" linaonesha kukatishwa kwa habari. Hapa msimuliaji anatoa taarifa juu ya Mikali.

Mikali

Alikuwa ni binti wa Mfalme Sauli na pia mke wa kwanza wa Daudi.

alimdharau moyoni mwake

Hapa "moyo" unawakilisha mawazo na hisia. Yaani: "alimwangalia kwa dharau"

mbele za Yahwe

"kwa Yahwe"

2 Samuel 6:18

aliwabariki watu kwa jina la Yahwe wa majeshi

Kubariki "katika jina la Yahwe wa majeshi" inamaanisha kubariki kwa nguvu na mamalaka ya Yahwe, au kama mwakilishi wake.

keki ya zabibu kavu

mkate mtamu uliookwa kutokana na zabibu kavu

2 Samuel 6:20

Mikali

Ni jina la mke wa kwanza wa Daudi.

ondoka

Hapa "alikuja" laweza kufasiriwa kama "kwenda."

Jinsi gani mfalme wa Israeli alivyokuwa mtukufu leo.

Hii ni aina ya usemi. Mikali anamaanisha kinyume cha kile alichosema, na haamini Daudi alitenda kwa heshima. Mikali anazungumzia kucheza kwa Mfalme Daudi na mwenendo wake bila heshima.

mbele ya wacho ya wajakazi

Hapa "macho ya wajakazi" inawakilisha wajakazi. Yaani: "mbele ya wajakazi"

mpumbavu

Daudi analinganishwa na mtu asiye na adabu na mpumbavu.

2 Samuel 6:21

aliyenichagua juu ya baba yako

Hapa "yako" inarejerea kwa Mikali.

juu ya watu wa Yahwe, Israeli

Hapa "juu ya watu wa Yahwe" na "Israeli" inamaanisha kitu kimoja.

nitakuwa hata zaidi nisiyefaa kuliko hivi

Daudi anatumia usemi wa kumaanisha kinyume chake. Haamini kwamba alichokifanya hakikuwa na heshima au kwamba matendo yake yatakuwa hayaheshimiwi.

Nitajishusha mbele ya macho yangu mwenyewe

Hapa "katika macho yangu mwenyewe" inawakilisha anachofikiri mtu au kufikiri juu ya kitu fulani. Yaani: "nitajihesabu mimi mwenyewe si kitu"

Lakini kwa hawa wajakazi uliowasema, nitaheshimiwa.

Hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji. Yaani: "Lakini wajakazi uliowasema wataniheshimu"

hakuwa na watoto hata siku ya kufa kwake

"hakuwa na uwezo wakuzaa watoto hata siku ya kufa kwake"

2 Samuel 7

2 Samuel 7:1

Ikawa

Kifungu kinaonesha mwanzo wa habari nyingine.

alipewa kupumzika kutokana na adui wote waliomzunguka

"kupewa usalama kutokana na adui wote waliomzunguka." Hapa "pumziko" ni jina dhahania. Yaani: "kusababisha makundi ya maadui kuacha kushambulia Israeli"

Ninaishi katika nyumba ya mwerezi

Mwerezi ni aina ya mti unaojulikana kwa uimara. Ni sawa na mninga katika utamaduni wetu. Inaaweza kuwa: "Ninaishi katika nyumba nzuri na ya kudumu"

sanduku la Mungu linakaa katikati ya hema

Hema ni makazi ya muda. Yaani: sanduku la Mungu lakaa katika eneo la muda"

2 Samuel 7:3

fanya lililomo moyoni mwako

Hapa "moyo" unawakilisha akili. Yaani: "fanya unalofikiri linapaswa kufanyika"

maana Yahwe yupo nawe

Hapa "pamoja nawe" linamaanisha Mungu anamsaidia na kumbariki Daudi.

neno la Yahwe lilikuja

Hii ni aina ya usemi kumaanisha kwamba Yahwe alisema. "Yahwe alisema ujumbe"

neno la Yahwe

Hapa "neno" linawakilisha ujumbe wa Yahwe

na akasema, "Nenda na umwambie Daudi mtumishi wangu, 'Hivi ndivyo asemavyo Yahwe: Je wewe utanijengea nyumba ya kuishi?

Hii ina nukuu ndani ya nukuu. Yaani: "na kusema, "Nenda na umuulize Daudi kama anadhani atakuwa ndiye wa kunijengea nyumba nitakayoishi."

Je wewe utanijengea nyumba ya kuishi?

Yahwe anatumia nukuu kusisitiza kwamba Daudi hatajenga nyumba kwa ajili ya Yahwe. Nukuu hii inaweza kufasiriwa kama taarifa. Yaani: "Hautanijengea nyumba ya kuishi"

kunijengea nyumba

Hapa nyumba inamaanisha hekalu. Katika 7:11 Yahwe atasema kwamba atamjengea Daudi nyumba. Pale "nyumba" inamaanisha familia.

2 Samuel 7:6

Je niliwai kusema jambo lolote kwa kiongozi yeyote wa Israeli niliyemchagua kuwachunga watu wangu Israeli, kusema, "Kwa nini hamjanijengea nyumba ya mwerezi?

Hii ina nukuu ndani ya nukuu nyingine. Nukuu ya moja kwa moja inaweza kuelezwa kama nukuu isiyo ya moja kwa moja. Yaani: "Sijawai kumwambia mmojawapo wa viongozi, niliowachagua, kunijengea hekalu la mbao za mwerezi."

Je niliwai kusema jambo lolote kwa kiongozi yeyote wa Israeli

Yahwe anatumia nukuu kusisitiza kwamba hakuwai kuwambia viongozi wa Israeli kumjengea nyumba.

Kwa nini hamkuwai kunijengea nyumba ya mwerezi?

Ikiwa Yahwe alikuwa amewauliza viongozi swali hili, angekuwa ametumia swali kuwalaumu kwa kutomjengea nyumba ya mwerezi. Lakini, Yahwe alisema hapo mwanzo kwamba hakuwa amewauliza swali hili. Yaani: "Mlipaswa kuwa mmenijengea nyumba ya mwerezi."

niliowateua kuwachunga watu wangu Israeli

Viongozi wanasemwa kama wachungaji na watu kama kondoo.

2 Samuel 7:8

Maelezo kwa Jumla

Yahwe anafafanua ahadi zake kwa Mfalme Daudi kupitia nabii Nathani.

Basi

Hii haimaanishi "sasa," lakini imetumika kuonesha utayari kwa jambo mhimu lifuatalo.

mwambie mtumishi wangu Daudi, "Hivi ndivyo asemavyo Yahwe wa majeshi: 'nilikutoa...jina kuu kwa ajili yako, kama jina la wakuu waliopo juu ya nchi.

Hii inanukuu ndani ya nukuu. Yaweza kufasiriwa: "mwambie Daudi mtumishi wangu kwamba nilimtoa... jina kuu kwa ajili yake, kama jina la mojawapo wa watu wakuu waliopo duniani"

mwambie Daudi mtumishi wangu

Yahwe bado anamwambia nabii Nathani anachopaswa kumwambia Daudi.

nimekuwa pamoja nawe

Hapa "pamoja nawe" inamaanisha kwamba Yahwe amemsaidia na kumbariki Daudi.

na nimewaondoa adui zako wote

Yahwe aliwaaribu adui wa Daudi inazungumzwa kana kwamba Yahwe aliowaondolea mbali, kama ambavyo mtu angekata vipande vya nguo au tawi kutoka katika mti.

kufanya jina kuu kwa ajili yako

Hapa "jina" inawakilisha heshima ya mtu.

kama jina la wakuu waliopo duniani

Kifungu "wakuu" inamaanisha watu mashuhuri.

2 Samuel 7:10

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kueleza ahadi zake kwa Mfalme Daudi kupitia nabii Nathani.

Nitateua mahali

"Nitachagua sehemu"

nitawapanda pale

Yahwe anawafanya watu waishi katika nchi daima na kwa usalama inazungumzwa kama kama angewapanda katika nchi.

na hawatasumbuliwa tena

Hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji: Yaani: "na hakuna atakayewasumbua tena"

kutoka siku

Hapa "siku" inawakilisha kipindi kirefu.

Niliwaamru waamzi

Baada ya Waisraeli kuingia katika nchi ya Kanaani na kabla ya kuwa na wafalme wa kuwatawala, Mungu aliteua viongozi walioitwa "waamzi" kuwaongoza katika nyakati za shida.

Nami nitakupa pumziko kutoka kwa adui zako wote...anakwambia kwamba atakutengenezea nyumba

Yaweza kufasiriwa: "Nami nitampa pumziko kutoka kwa adui zake wote... anamwambia kwamba atamtengenezea nyumba"

Nikupumzisha kutoka kwa adui zako wote

"Nitakupa usalama kutoka kwa adui zako wote." Hapa "pumziko" ni nomino dhahania. Yaweza kuwa: "Nitawafanya adui zako wote waache kukushambulia"

Nitakutengenezea nyumba

Maana hii hapa ya "nyumba" inarejea kwa wazao wa Daudi kuendelea kumiliki katika Israeli. Katika 7:3 Yahwe alimuuliza Daudi ikiwa angemjengea nyumba. Pale "nyumba" inawakilisha hekalu.

2 Samuel 7:12

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kueleza ahadi zake kwa Mfalme Daudi kupitia nabii Nathani.

Siku zako zitakapokamilika na ukalala na baba zako

Vifungu hivi viwili vina maana sawa na vimeunganishwa kwa msisitizo. Vyote ni njia ya nyepesi ya kuonesha kifo na kufa.

Nitainua mzao baada yako

Yahwe aliteua mzao wa Daudi inaoneshwa kama Yahwe angeinua juu.

atakaye toka katika mwili wako

Usemi huu unamaanisha kwamba mtu huyo atakuwa mzao wa Daudi.

Nitauimarisha ufalme wake

Hapa "ufalme wake" inawakilisha nguvu ya kumiliki.

nyumba kwa jina langu

Hapa "jina" renarejea kwa Yahwe. Yaani: "makazi yangu ya kudumu"

Nitakifanya imara kiti cha enzi cha ufalme wake daima.

Hapa "kiti cha enzi" inawakilisha nguvu ya mtu kumilki kama mfalme.

Nitakuwa baba kwake, naye atakuwa mwanangu

Unabii katika 7:12-14 unarejea kwa Sulemani, mwana wa Daudi. Lakini, mambo ya unabii yatatimizwa na Yesu.

2 Samuel 7:15

Maelezo ya Jumla

Yahwe alimaliza kueleza ahadi zake kwa Mfalme Daudi kupitia nabii Nathani.

Lakini umaminifu wangu wa kiagano hautamwacha, kama nilivyomwondolea Sauli

Neno "uaminifu" ni jina dhahania linaloweza kuelezwa kama "aminifu." Lakini pia taarifa hii yaweza kufasiriwa katika muundo chanya. Yaani: "Lakini nitabaki mwaminifu kwake, tofauti na nilivyokuwa kwa Sauli"

kutoka mbele yako. Nyumba yako... mbele yako. Kiti chako cha enzi

Hapa "wewe" inarejea kwa "Daudi". "kutoka mbele ya Daudi. Nyumba ya Daudi... mbele yake. Kiti chake cha enzi"

Nyumba yako na ufalme wako utathibitishwa daima mbele yako. Kiti chako cha enzi kitasimamishwa daima.

Sentensi hizi mbili zinamaana sawa na zinasisitiza nasaba ya Daudi kutawala daima.

Nyumba yako na ufalme wako utaimalika daima mbele yako

Hapa neno "nyumba" inawakilisha uzao wa Daudi, watakao tawala kama wafalme. Hapa "ufalme" humaanisha jambo lilelile kama "nyumba." Utaona nikiimalisha familia yako na utawala wao juu ya watu wa Israeli daima"

Kiti chako cha enzi kitakuwa imara daima

Hapa "kiti cha enzi" kinawakilisha nguvu ya kutawala kama mfalme.

maneno haya yote

Hapa "maneno" yanawakilisha kile alichokisema Yahwe.

Alimwambia kuhusu ono lote

"Alimwambia kuhusu kila kiti Yahwe aliyomwonesha"

2 Samuel 7:18

Mimi ni nani, Yahwe Mungu, na familia yangu ni nini hata umenileta katika kiwango hiki?

Daudi anauliza swali hili kuonesha hisia za ndani alizozihisi baada ya kusikia tamko ya Yahwe. Swali hili lisiloitaji jibu laweza kufasiriwa: "mimi na familia yangu hatusitahili heshima hii, Yahwe Mungu."

Hili lilikuwa jamba dogo mbele yako

Hapa "mbele yako" inawakilisha alichokikusudia Yahwe kiwe.

familia ya mtumishi wako

Hapa Daudi anajirejerea kama "mtumishi wako."

Kwa kitambo kijacho

Hii inaongelea wakati kama kitu fulani kisafiricho na kuwasili mahali fulani.

Nini zaidi, Mimi Daudi naweza kukwambia?

Daudi anatumia swali hili kusisitiza kwamba hana kilichaobaki cha kumwambia Yahwe.

mtumishi wako

Hapa Daudi anajirejerea kama "mtumishi wako." Hii yaweza kuelezwa katika nafsi ya kwanza

2 Samuel 7:21

Kwa ajili ya neno lako

Hapa "neno" linawakilisha alikiahidi Mungu.

kutimiza kusudi lako mwenyewe

"kukamilisha ulichopanga kufanya"

kwa mtumishi wako

Daudi anajirejerea kama "mtumishi wako."

Kama tulivyosikia kwa masikio yetu

Kifungu "kwa macho yetu wenyewe" inatumika kwa msisitizo.

Kama tulivyosikia

Hapa "sisi" inamwonesha Daudi na taifa la Israeli.

Na ni taifa gani lililo kama watu wako Israeli, taifa pekee juu ya dunia ambalo wewe, Mungu, ukikwenda na kukikomboa kwa ajili yako mwenyewe?

Daudi anatumia msisitizo wa swali kwamba hakuna taifa lingine kama Israeli. Yaani: "Hakuna taifa lililo kama watu wako Israeli, taifa moja juu ya nchi ambalo wewe, Mungu, ulikwenda na kulikomboa kwa ajili yako."

Kijifanyia jina wewe mwenyewe

Hapa "jina" inawakilisha heshima ya Yahwe.

kwa nchi yako

Hapa "nchi" inawakilisha watu.

Uliyaondoa mataifa

Hapa "mataifa" inawakilisha makundi ya watu waliokuwa wakiishi Kanaani.

2 Samuel 7:24

Maelezo ya Jumla

Daudi aliendelea kuongea na Yahwe.

Hivyo basi

Hapa "basi" haimaanishi "sasa," lakini inatumika kuleta usikivu kwa jambo muhimu kama ifuatavyo.

Na ahadi uliyoifanya kuhusu mtumishi wako na familia yake iwe imara daima

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. Yaani: "Na ufanye ulichoniahidi na familia yangu, na ahadi yako isibadilike"

mtumishi wako na familia yake

Daudi anajisema katika nafsi ya tatu. Yaweza kuwa: "mimi na familia yangu"

Jina lako na liwe kuu daima

Hapa "jina" inawakilisha heshima ya Yahwe.

Nyumba yangu, Daudi, mtumishi wako

Hapa "nyumba" inawakilisha familia.

Umethibitishwa mbele yako

Hii yaweza kuwa "ni salama kwa sababu wewe" au "unaendelea kwa sababu yako"

2 Samuel 7:27

kwa mtumishi wako kwamba utamjengea nyumba

Daudi anajirejerea kama "mtumishi wako"

kwamba utamjengea nyumba

Hapa aina hii ya usemi "nyumba" inarejea kwa uzao wa Daudi kuendelea kuwa watawala wa Israeli. Katika 7:3 Yahwe alimwambia Daudi kama angekuwa mjenzi wa nyumba ya Yahwe. Hapa "nyumba" inawakilisha hekalu.

Basi

Hii haimaanishi "sasa," lakini inatumika kutoa angalizo kwa jambo mhimu lifuatalo.

maneno yako ni ya kuaminika

Hapa "maneno" yanawakilisha anachosema Yahwe. Yaani: "Ninaamini ukisemacho"

na kwa baraka yako nyumba ya mtumishi wako itabarikiwa daima

Hii inaweza kutaarifiwa kwa muundo tendaji. Yaani: "na utaendelea kuibariki familia yangu daima.

nyumba ya mtumishi wako

Hapa Daudi anajirejerea mwenyewe kama "mtumishi wako." Yaani: "nyumba yangu" au "familia yangu"

nyumba

Hapa "nyumba" inawakilisha familia ya Daudi.

2 Samuel 8

2 Samuel 8:1

Daudi akashambulia

Hapa Daudi anawakilisha askari wake.

2 Samuel 8:2

Kisha akashinda

Hapa "yeye" inarejea kwa Daudi anayewakilisha askari wake.

akawapima watu wakekwa mstari... akapima mistari miwili ya kuuwa, na mstari mmoja kamili wa kuacha hai.

Hapa "mstari" ni "kamba." Daudi aliwafanya askari walale chini ili wapimwe na kuwekwa katika makundi matatu. Waliokuwa katika makundi mawili waliuawa, na katika la tatu, waliachwa hai.

2 Samuel 8:3

Kisha Daudi akamshinda Hadadezeri

Hapa wote "Daudi" na "Hadadezeri" wanawakilisha majeshi yao. "Daudi na jeshi lake walimshinda Hadadezeri na jeshi lake"

Hadadezeri... Rehobu

Haya ni majina ya wanaume.

Soba

Hili ni jina la jimbo katika Shamu.

Kuurudisha ufalme wake

"Kurudisha utawala juu ya mkoa" au "kulishika tena mkoa"

askari wa miguu ishirini elfu

"20,000 watu wa miguu"

Daudi akawakata miguu

Hili ni tenda ambapo sehemu ya nyuma ya miguu inakatwa ili farasi wasiweze kukimbia.

kutunza ya kutosha

"kutenga ya kutosha" au kutunza ya kutosha"

vibandawazi mia moja

"vibanda wazi 100"

2 Samuel 8:5

Daudi akaua

Hapa Daudi anawakilisha askari wake.

Washami elfu ishirini

washami 22,000

Akaweka ngome huko Shamu

"aliagiza kundi kubwa la askari wake kubaki Shamu"

2 Samuel 8:7

Daudi akachukua... Mfalme Daudi akachukua

Hapa Daudi anawakilisha askari wake.

Beta na Berothai

Haya ni majina ya mahali.

2 Samuel 8:9

Tou...Hadoramu

Haya ni majina ya wanaume.

Hamathi

Hili ni jina la mahali.

Daudi alishinda

Hapa "Daudi" inawakilisha jeshi lake.

2 Samuel 8:11

na Amaleki

"na Waamaleki"

Vitu vilivyotekwa

Hivi ni vitu vya thamani askari wanavyoviteka kutoka kwa walioshindwa.

Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba

Hili ni jina la mfalme wa Soba

2 Samuel 8:13

Jina la Daudi likajulikana sana

Hapa "jina" linarejea kwa heshima ya Daudi. Yaani "Daudi alikuwa maarufu sana"

Bonde la chumvi

Hili ni jina la mahali. Mahali pake kabisa hapafahamiki.

Watu elfu themanini.

"watu 18,000"

Akaweka ngome katika Edomu yote.

"Aliagiza makundi ya askari wake kubaki katika maeneo yote ya Edomu"

2 Samuel 8:15

Yoabu mwana wa Seruya

Hili ni jina la mwanaume

Ahiludi... Ahitubu... Ahimeleki... Seraya... Yehoiada

Haya ni majina ya wanaume.

Ahiludi alikuwa mwenye kuandika taarifa.

Mwandishi alikuwa mtu aliyekuwa akiongea na watu na kuwambia matangazo ya mfalme.

Wakerethi... Wapelethi

Haya ni majina ya makundi ya watu. Hawa walikuwa walinzi wa Daudi.

2 Samuel 9

2 Samuel 9:1

Kwa ajili ya Yonathani

"kwa sababu ya upendo wangu kwa Yonathani"

Kwa ajili ya Yonathani

Yonathani alikuwa mwana wa Sauli na rafiki wa karibu sana wa Daudi.

Siba

Hili ni jina la mwanaume.

Mimi ni mtumishi wako

Siba anajiita "mtumishi wako" kuonesha heshima kubwa kwa Daudi.

2 Samuel 9:3

Ninaweza kuonesha ukarimu wa Mungu

Yaweza kufasiriwa kuwa "naweza kuwa mkarimu kama niliyomwaidi Mungu"

mlemavu katika miguu yake

"Ambaye miguu yake imearibika." Neno "miguu" hapa linaonesha uwezo wa kutembea.

Makiri... Amieli

Haya ni majina ya wanaume.

Lo Debari

Hili ni jina la sehemu.

2 Samuel 9:5

Mfalme Daudi akatuma

Inafahamika kwamba Daudi alituma wajumbe.

Mefiboshethi

Hili ni jina la mwanaume

alikuja kwa Daudi

Neno "alikuja" laweza fasiriwa kuwa "alikwenda."

Mimi ni mtumishi wako

Mefiboshethi anajirejerea kama "mtumishi wako" kuonesha heshima kubwa kwa mfalme.

2 Samuel 9:7

Kwa ajili ya Yonathani baba yako

"Kwa sababu nilimpenda baba yako, Yonathani"

Utakula daima katika meza yangu.

Hapa "meza" inawakilisha kuwa pamoja na Daudi katika uwepo. Kula na mfalme mezani ilikuwa ni heshima kubwa.

Mtumishi wako ni nini, hata umwangalie kwa upndeleo mbwa mfu kama mimi?

Swali hili lisiloitaji jibu laonesha kuwa Mefiboshethi anafahamu kuwa hana umuhimu wowote wa mfalme kumjari.

mbwa mfu huyo

Hapa Mefiboshethi anawakilisha uzao wa Sauli, na anajilinganisha na "mbwa mfu." Mbwa walikuwa wanyama wasioheshimiwa, mbwa mfu alikuwa hana umuhimu kabisa.

2 Samuel 9:9

Ni lazima ale Daima katika meza yangu

Hapa "meza yangu" inawakilisha kuwa pamoja na Daudi.

Basi Siba... watumishi

Hapa "basi" inaonesha mkato wa habari. Msimuliaji anatoa taarifa kuhusu Siba.

wana kumi na watano na watumishi ishirini

"wana 15 na watumishi 20"

2 Samuel 9:11

Mtumishi wako atafanya yote ambayo bwana wangu mfalme amemwagiza mtumishi wake

Siba anajitaja kama "mtumishi wako" na kumtaja Daudi kama "bwana wangu". Mtumishi wako atafanya yote ambayo wewe bwana wangu mfalme umeagiza.

Mika

Hili ni jina la mwana wa Mefiboshethi.

wate walioishi katika nyumba ya Siba

Hapa "nyumba" inawakilisha familia ya Siba.

Anakula katika meza ya mfalme daima

Hapa "meza" inawakilisha kuwa pamoja na Daudi au katika uwepo wake.

Japokuwa alikuwa kilema katika miguu yote miwili.

Hakuweza kutembea.

2 Samuel 10

2 Samuel 10:1

Hanuni...Nahashi

Haya ni majina ya wanaume

Je unadhani...wewe?

Viongozi wanatumia swali kushauri kwamba mfalme asimwamini Daudi.

Kupeleleza

Kutafuta habari kuhusu mtu fulani kwa siri.

Je Daudi haja...uteka?

Viongozi wanatumia swali kushauri kwamba mfalme asimwamini Daudi.

Ili kuupindua

Hapa "huo" inarejea kwa mji ambao unawakilisha watu walioishi pale.

mji

Hapa "mji" inahusu Raba, mji mkuu wa Waamoni.

2 Samuel 10:4

kunyoa ndevu nusu ya zao

Inamaanisha tusi la kuwadharirisha watu.

walikuwa wameaibika sana

Hapa "kwa kina" ni usemi unaomaanisha "sana"

Kisha mrudi

Inamaanisha kwamba watapaswa kurudi Yerusalemu

2 Samuel 10:6

wakawa harufu mbaya kwa Daudi

Kifungu "kuwa harufu mbaya" inamaanisha kuwa chukizo

Beth Rehobu... Soba... Maaka... Tobu

Haya ni majina ya mahali.

Elfu ishirini... elfu... elfu kumi na mbili

"20,000... 1,000...12,000"

kwa langu la mji wao

Hapa "mji" inarejea kwa Raba, mji mkuu wa Waamoni

2 Samuel 10:9

Maelezo ya Jumla

Vita na ya Washami na Amoni inaendelea.

Na kwa sehemu ya jeshi iliyosalia, akaiweka chini ya mamlaka ya Abishai nduguye.

"Akamweka Abishai nduguye mkuu wa jeshe lililosalia"

2 Samuel 10:11

Maelezo ya Jumla

Yoabu analiweka tayari jeshi kwa vita.

Kwangu, kisha wewe, Abishai, lazima uniokoe

Hapa "mimi" inarejea kwa Yoabu anayewakilisha askari wake. Pia, Abishai anawakilisha jeshi lake.

2 Samuel 10:13

Kutoka kwa Abishai

Hapa Abishai anawakilisha askari wake.

Ndani ya mji

Hapa "Mji" unahusu Raba, makao makuu ya Waamaoni.

Na kurudi Yerusalemu

"na kurudi Yerusalemu

2 Samuel 10:15

Washami walipoona kwamba wameshindwa na Israeli

Hii yaweza kufasiriwa kama: "Washami walipotambua kuwa Waisraeli walikuwa wanawashinda"

Hadadezeri... Shobaki

Haya ni majina ya wanaume.

kutoka ng'ambo ya Mto Frati

Hii inamaanisha upande wa mashariki wa Mto Frati.

Walikuja kwa Helamu

Hapa "walikuja kwa" yaweza kufasiriwa kuwa "walikwenda kwa" au "walikutanika kwa"

Helamu

Hili ni jina la sehemu.

katika kichwa chao

Kifungu hiki kinaoneshwa nafasi ya mamlaka.

2 Samuel 10:17

Daudi alivyoambiwa hiki

Inamaanisha "Daudi aliposikia kuhusu hili"

Kusanya Isreali wote pamoja

Hapa "Israeli" inawakilisha jeshi la Israeli.

Helamu

Jina la mahali

Kinyume na Daudi na kupigana naye

Hapa Daud anawakilisha askari wake.

Daudi aliua

Hapa Daudi anawakilisha askari wake.

Mia saba... elfu arobaini

"700... 40,000"

Shobaki jemedari wa jeshi lao alijeruhiwa na kufa pale

Hii yaweza kufasiriwa: "Waisraeli walimjeruhi Shobaki jemedari wa jeshi wa Washami, na akafa pale"

Shobaki... Hadareza

Haya ni majina ya wanaume.

waliona kwamba walikuwa wameshindwa na Israeli

Yaweza kufasiriwa kuwa " walitambua kuwa Waisraeli walikuwa wamewashinda"

2 Samuel 11

2 Samuel 11:1

Ikawa wakati wa majira ya kipupwe

"Ilitokea wakati wa majira ya kipupwe." Hii inatambulisha tukio jingine katika habari.

katika wakati

"wakati wa mwaka"

Daudi akampeleka Yoabu, watumishi wake, na jeshi lote la Israeli

Daudi aliwapeleka waende vitani.

Jeshi la Amoni

"Jeshi la Waamoni"

Raba

Hili ni jina la mji.

2 Samuel 11:2

Hivyo ikawa

"Hivyo ikatokea" au "Hivyo ikatendeka". Mwandishi anatumia kifungu hiki kutambulisha tukio jipya katika habari.

Hivyo Daudi akatuma

Hapa neno "tuma" linamaanisha Daudi alipeleka mjumbe.

Akawauliza watu ambao wangeweza kujua kuhusu mwanamke

Daudi alikuwa anajaribu kutafuta mwanamke yule alikuwa nani. Neno "yeye" inarejea kwa Daudi, lakini inamaanisha mjumbe aliyetumwa na Daudi. Alipaswa kuuliza habari kuhusu mwanamke.

Je siye Bethsheba... naye ni mke wa Uria Mhiti.

Swali hili linatoa taarifa na laweza kuandikwa kwa maelezo. Huyu ni Bathsheba... naye ni mke wa Uria Mhiti."

2 Samuel 11:4

Hezi

Kipindi cha mwanamke cha mwezi

na kumchukua

"na kumchukua." Daudi alimchukua mwanamke, lakini alikuwa mjumbe aliyekuwa ametumwa aliyemchukuwa na kumleta kwa Daudi.

Akaja kwake ndani, naye akalala naye

Kifungu "alikuja kwake ndani" inaonesha hali ya Daudi kufanya tendo la ndoa na mwanamke.

Alituma na kumwambia Daudi; akasema, "Niko mjamzito"

Hapa neno "alipeleka" linamaanisha kwamba alipeleka mjumbe kumwambia Daudi kwamba alikuwa mjamzito.

2 Samuel 11:6

Kisha Daudi akatuma

Hapa neno "kutuma" inamaanisha kwamba Daudi alituma mjumbe.

Yoabu anaendeleaje, jeshi linaendeleaje, na vita inaendeleaje

Daudi alikuwa akiuliza ikiwa Yoabu na jeshi walikuwa wanaendelea vema na kuhusu maendeleo ya vita.

Shuka nyumbani kwako

Maana pendekezwa kwa kifungu "shuka chini" ni 1) Nyumba ya Uria ilikuwa chini kuliko kasiri la Daudi au 2) Nyumba ya Uria ilikuwa na umuhimu mdogo kulinganisha na kasiri la mfalme.

Nawa miguu yako

Kifungu hiki kinamaanisha kurudi nyumbani kupumzika wakati wa usiku baada ya kufanya kazi mchana kutwa.

Mfalme alituma zawadi kwa Uria

Daudi alituma mtu kupeleka zawadi kwa Uria.

2 Samuel 11:9

Bwana wake

Neno "yake" inarejerea kwa Uria na neno "bwana" inarejerea kwa Daudi.

Je haujatoka safarini? Kwa nini haukwenda nyumbani kwako?

Hili swali linaonesha ushangao wa Uria kwa nini hakumtembelea mke wake.

Israeli na Yuda

Hii inarejea kwa majeshi yao yaani "majeshi ya Israeli na Yuda"

Jinsi gani basi mimi naweza kwenda kwangu... pamoja na mke wangu?

Swali hili linasisitiza hali ya Uria kukataa kumtembelea mke wake.

Kwa hakika kama uishivyo, sitafanya hivyo.

Uria anaapa kwa ahadi yenye nguvu kwamba hatakwenda nyumbani kwa mke wake kwa vile askari wengine wapo vitani.

2 Samuel 11:12

alikula na kunywa mbele yake

Uria alikula na kunywa na Daudi

chini katika nyumba yake

Maana pendekezwa hapa kwa neno "chini" 1) nyumba ya Uria ilikuwa chini ya ile ya Daudi. 2) nyumba ya Uria ilikuwa na umuhimu mdogo kuliko ile ya Daudi

2 Samuel 11:14

akaituma kwa mkono wa Uria

Kifungu "mkono wa Uria" inamrejea Uria mwenyewe.

Mbele kabisa ya vita vikali zaidi

"mbele zaidi ya vita mahali ambapo vita ni vikali sana"

Kumwacha

"Amru askari kurudi nyuma na kumwacha"

awe amepigwa na kuuawa

"Awe amejeruhiwa na kuuawa"

2 Samuel 11:16

Kuhusuru mji

Neno "kuhusuru" linaweza kuelezwa kwa kitendo "kuzingira" na "kushambulia". Yaani "jeshi lake lilizunguka na kuushambulia mki"

baadi ya askari wa Daudi walianguka

Neno "anguka" ni usemi laini wa kuonesha askari waliouawa. Yaani "baadhi ya askari wa Daudi waliuawa.

Na Uria Mhiti aliuawa pale

Inamaanisha "Uria Mhiti naye alikuwa miongoni mwao.

2 Samuel 11:18

Yoabu alituma neno kwa Daudi

"Kutuma neno" kunamaanisha kuwa alituma mjumbe kutoa taarifa kwa Daudi

Kwa nini mlikaribia hivyo... kutoka katika ukuta?

Yoabu anasema kwamba Daudi anaweza kumkemea kwa kuuliza swali hili. Yaweza kuwa "Hamkupaswa kuwa mmeukaribia mji hivyo ili kupigana nao. Kwani wangeweza kurusha mishale kutokea ukutani"

Piga kutoka ukutani

Inaonesha watu wa mji wakirusha mishale kwa adui wao kutokea ukutani.

2 Samuel 11:21

Ni nani aliyemwua Abimeleki mwana wa Yerubeshethi?

Yoabu anasema Daudi anaweza kumkemea kwa kuuliza swali hili. Yafaa kuwa "Kumbuka jinsi Abimeleki mwana wa Yerubeshethi alivyouawa!"

Abimeleki mwana wa Yerubeshethi

Hili ni jina la mwanaume. Babaye anajulikana pia kwa jina la Gideoni.

Je mwanamke hakurusha jiwe la juu la kusagia juu yake kutoka ukutani hivyo kwamba alikufa katika Thebezi?

Yoabu anasema Daudi aweza kumkemea kwa kuuliza swali. Yafaa kuwa "Kumbuka alikufa huko Thebezi mwanamke aliporusha jiwe la juu la kusagia juu yake kutokea ukutani"

kutokea ukutani

"kutokea juu ya ukuta wa mji"

Jiwe la kusagia nafaka

Jiwe zito ambalo lingeweza kuzunguka, lililotumika kwa kusaga nafaka ili kutengeneza mkate

Thebezi

Hili ni jina la mji.

Kwa nini mliukaribia ukuta kiasi hicho?

"Hamkupaswa kuwa mmeukaribia ukuta kiasi hicho!"

2 Samuel 11:22

lango

"lango la mji"

2 Samuel 11:24

Warusha mishale wao warusha

"Walirusha mishale"

Baadhi ya watumishi wa mfalme waliuawa

"Waliwauwa baadhi ya watumishi wa mfalme"

Mtumishi wako Uria Mhiti ameuawa

"Walimwua mtumishi wako Uria pia"

Watumishi wa mfalme

Hapa "watumishi" inarejerea askari, siyo watumwa, kwa sababu askari walikuwa watumishi wa mfalme.

Maana upanga hula huyu kama ulavyo mwingine.

Hapa "upanga" inarejerea kwa mtu anayemwua mwingine kwa upanga. Kumwua mtu kwa upanga unazungumzwa kama vile ni "kula" watu.

Ongezeni mashambulizi

"Piganeni kwa nguvu zaidi"

2 Samuel 11:26

Aliomboleza kwa kina

Hapa mwandishi anazungumza maombolezo yake kama yalikuwa ndani yake zaidi.

Huzuni

Hisia kali ya huzuni iliyosababisha maumivu, kukata tamaa au matatizo

Daudi alituma na kumchukua nyumbani

Hapa neno "tuma" linamaanisha alituma mjumbe kumchukua na kumleta kwake.

Kutopendezwa

"aliyehuzunishwa" au "kasirishwa"

2 Samuel 12

2 Samuel 12:1

kondoo jike

kondoo jike

alikuwa kama binti kwake

Hii inaonesha ukaribu wa mtu huyu na kondoo wake mdogo.

2 Samuel 12:4

Mtamba wa kondoo

Kondoo jike

Hasira ya Daudi ikawaka kinyume cha

Hapa mwandishi anaeleza jinsi Daudi alikuwa na hasira sana kama vile mwili wake ulikuwa umechemka kwa sababu ya hasira.

Mgeni wake

Ilikuwa ni kwa ajili ya chakula cha mgeni wake

Akamwambia Nathani kwa hasira

Hii inamaanisha kwamba Daudi aliongea na Nathani kwa hasira.

Kama Yahwe aishivyo

Hii inaeleza kwamba Daudi alikuwa akiapa kiapo au ahadi ya kuaminika.

Kumwua

Hii inamaanisha kumwua. Yaani kufa

Anapaswa kulipa kondoo mara nne

Kiasi tajiri alichopaswa kulipa kilikuwa mara nne ya thamani ya kondoo.

Huruma

Kujisikia huzuni na upendo kwa anayeumia au kutopendwa

2 Samuel 12:7

Kutoka mkononi mwa Sauli

Hapa neno "mkono" linaonesha utawala. Yaani "kutoka katika utawala wa Sauli"

wake za bwana wako katika mikono yako

Hapa Yahwe anaeleza Daudi akiwa na wake za bwana wake kama wake wake mwenyewe, kwa kusema kwamba wako "mikononi mwako."

Pia nilikupa nyumba ya Israeli na Yuda

Hapa Yahwe anaongelea jinsi alivyompa Daudi mamlaka yake kama mfalme juu ya Israeli na Yuda kama vile alimpa nyumba ya Israeli na Yuda. Kifungu "nyumba ya" kinamaanisha "watu wa."

Ikiwa hayo yangekuwa machache kwako

"Ikiwa nisingekupa vya kutosha"

2 Samuel 12:9

Hivyo kwa nini umedharau... Yahwe, hata kufanya maovu mbele zake?

Swali hili linatumika kumkemea Daudi. Yaani "haukupaswa kumdharau ... Yahwe na kufanya yaliyomaovu mbele zake!"

Hata kufanya yaliyomaovu mbele zake

"Mbele" ya Yahwe inarejea kwa kile anachofikiri. Hii inazungumzia anachohesabu kuwa uovu halisi.

Umemwua Uria Mhiti kwa upanga

Daudi hakumwua Uria kwa mkono wake, bali alipanga Uria alivyouawa. Kifungu "kwa upanga" kinaonesha jinsi alivyokufa vitani.

Ulimwua kwa upanga wa jeshi la Amoni

Inaonesha kwamba Daudi hakumwua kwa mkono wake bali alipanga jinsi ya kuuawa kwa Uria mkononi mwa Waamoni.

Upanga hautaondoka nyumbani mwako

Hapa neno "upanga" linaonesha watu wanaokufa vitani. "Nyumba" ya Daudi inarejerea wazawa wake.

2 Samuel 12:11

Katika nyumba yako mwenyewe

Hapa "nyumba" ya Daudi inarejerea kwa familia yake.

Mbele za macho yako

Hapa Daudi anarejerewa kwa kutajwa macho yake kusisitiza ambacho angeona.

mbele ya Israeli yote

Hapa inaonesha watu wote wa Israeli kujua juu ya kilichotendeka kwa wake zake kama vile wote walishuhudia tukio.

Wakati wa mchana

Wazo la kufanya jambo "hadharani" au katika njia ambayo watu wanafahamu kinachotendeka kama kinafanyika mchana.

Kutenda dhambi yako

"alitenda dhambi"

Kupita

Yahwe amesamehe dhambi ya Daudi. Hii inazungumzwa kama Yahwe anaipitisha dhambi kama kilikuwa kitu alichokipita na kutokukijari.

Hautakufa

Hatakufa kwa sababu ya kutenda dhambi hii na mwanamke.

2 Samuel 12:14

Kudharau

Kutokupenda au kumchukia mtu au kitu

Yahwe alimpiga mtoto... na akawa mgonjwa sana.

Yahwe anaonekana kusababisha ugonjwa wa mtoto kama vili amempiga.

mtoto aliyezaliwa kwako

Kifungu "kuzaliwa kwako" inamaanisha kwamba huyu ni mtoto wa Daudi

Mtoto ambaye mke wa Uria alimzalia Daudi

Hii inamaana kwamba alizaa mtoto ambaye Daudi ndo alikuwa baba yake.

2 Samuel 12:16

Kusihi

Kuombeleza au kuomba kwa hamu kubwa

kwenda ndani

Daudi alikwenda ndani ya chumba chake alipokuwa peke yake.

Kumwinua kutoka sakafuni

" na kumsihi kuinuka kutoka chini"

Ikawa

"Ilitokea"

Hakuisikiliza sauti yetu

Hapa "sauti" inasisitiza kwamba walikuwa wakiongea.

Siku ya saba

Hii ni siku ya saba tangu mtoto azaliwe

Tazama

Usemi unatumika kuwafanya watu wawe "makini"

Je atajitendeaje ikiwa tutamwambia kwmba mtoto amekufa?!

Watumishi wanauliza swali hili kuonesha hofu yao. Yaani "tunaogopa kwamba anaweza kujidhuru ikiwa tutamwambia kwamba mtoto amekufa!"

2 Samuel 12:19

Kunong'oneza

"kuongea polepole sana"

Kutambua

"Kuelewa"

Inuka

"simama juu"

2 Samuel 12:21

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ina maswali yasiyoitaji majibu msisitizo ambao Daudi anatambua kwamba Yahwe ameruhusu hili kutendeka.

Nani ajuaye kuwa Yahwe atanirehemu, ili mtoto aishi?

Daudi anauliza swali hili kusisitiza kwamba hakuna ajuaye kama Yahwe angemwacha mtoto aishi. Hii inaweza kuandikwa kama taarifa. Hakuna ajuaye kwamba Yahwe atanirehemu ili mtoto aishi.

Lakini sasa amekufa, hivyo kwa nini nifunge?

Daudi anatumia swali hili kutoa msisitizo kwamba hana haja ya kufunga tena.

Je naweza kumrudisha tena?

Daudi anatumia swali hili kutoa msisitizo kwamba mtoto hawezi kurudi kuwa hai.

Nitakwenda kwake

Daudi anaonesha kwamba atakapokufa atakwenda kwa mtoto.

2 Samuel 12:24

Akaingia kwake, na kulala naye

Kifungu "kuingia kwake" ni tamathali ya kuonesha kwamba Daudi alifanya tendo la ndoa na mkewe. Vifungu hivi viwili vinamaana moja na vinatumika kusisitiza kwamba walilala pamoja.

Alituma neno kupitia nabii Nathani

Hapa "neno" inarejerea kwa Yahwe aliyemwambia Nathani kumwambia Daudi.

Yedidia

Hili ni jina lingine la Sulemani mwana wa Daudi, Yahwe alilolichagua kwa ajili yake.

2 Samuel 12:26

Yoabu akapigana... akaukamata

Hapa mwandishi anasema "Yoabu" lakini anarejerea kwa Yoabu na askari waliopigana pamoja naye.

Raba

Kupigana dhidi ya mji hu, halisia inamaanisha kupigana dhidi ya watu wa Raba.

Hivyo Yoabu akatuma wajumbe kwa Daudi na kusema

"Hivyo Yoabu akatuma wajumbe kwa Daudi kumwambia"

Wamechukua sehemu ya kusambaza maji mjini

"Kukamata" eneo inamaanisha kuchukua umilki.

Kupiga kambi kinyume

Hii inamaanisha kuzunguka na kushambulia.

Nimepigana... nimekamata... ikiwa nitachukua

Hapa Yoabu anajisemea mwenyewe wakati halisia anarejerea kwake na askari wake.

Uchukue... chukua mji

"Kuchukua" eneo inamaanisha kuchukua umilki.

Utaitwa

Hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji. Yaani "watu watauita"

2 Samuel 12:29

Alipigana

Hapa mwandishi anazungumzia Daudi wakati kwa uhalisia anarejerea kwa Daudi na askari wake.

Talanta

Kwa vipimo vya sasa ni sawa na "kilo 34"

Jiwe la thamani

Jiwe la nadra kupatikana kama vile almasi, rubi, na mengine

Taji iliwekwa katika kichwa cha Daudi mwenyewe

Waliweka taji katika kichwa cha Daudi.

Akaondoa

Hapa mwandishi anazungumzia Daudi wakati ki halisia anarejerea kwa askari wa Daudi.

Mateka

Vitu vya thamani vinavyochukuliwa kutoka kwa adui aliyeshindwa.

Kwa wingi

"kiwango" au "idadi"

2 Samuel 12:31

Akawaleta watu nje

Daudi hakuwaleta nje watu mwenyewe; aliwaagiza askari wake kuwaleta nje.

misumeno, sululu, na shoka

Hivi ni vifaa vya kukata miti au kuvuja ardhi.

Sehemu ya kutengenezea matofali

Sehemu ambapo matofali yanakausha na kufanywa magumu

Miji yote ya watu wa Amoni

Hii inarejerea kwa watu katika mji.

2 Samuel 13

2 Samuel 13:1

Ikawa baada ya haya

"Ilitukia baada ya haya." Kifungu hiki inatambulisha tukio jipya katika habari.

Dada wa kambo

Amnoni na Tamari walikuwa watoto wa baba mmoja lakini mama tofauti

Dada

Absalomu na Tamari walikuwa watoto wa baba na mama mmoja.

Amnoni alichanganyikiwa kiasi cha kuwa mgojwa kwa kwa sababu ya Tamari dada yake

Hii ni kwa sababu Amnoni alimtamani ili alale nae.

2 Samuel 13:3

Yehonadabu mwana wa Shama, nduguye Daudi

Haya ni majina ya wanaume. Shama alikuwa kaka wa Daudi.

Mwelevu

mwenye akili au mdanganyifu

Kuwa na mawazo

Ni hali ya kihisia au huzuni ya hali ya juu

Je hautaniambia?

Swali hili ni ombi la Yehonadabu ili aambiwe kwa nini Amnoni ana hali hiyo.

2 Samuel 13:5

Yehonadabu

Hili ni jina la mwanaume

Kujifanya kuugua

Kuwa na mwonekano wa kuwa mgonjwa

na kula kutoka mkononi mwake... niweze kula mkononi mwake

Hili ni ombi lake ili ahudumiwe chakula peke yake.

kwa ugonjwa wangu mbele yangu

Chakula si kwa ajili ya ugonjwa wake, bali ni kwa ajili yake kwa sababu ni mgonjwa. Kifungu "mbele yangu" ni ombi kwa kuandaa chakula mbele yake.

2 Samuel 13:7

Daudi akatuma neno

Hii inamaanisha kwamba alituma mjumbe kuongea na Tamari

Donge

Mchanganyiko wa unga na maji unaotumika kwa kuokea.

Kuukanda

Kutumia mikono kulichanganya donge

mbele yake

Hii inamaanisha kwamba Tamari alitengeneza mkate mbele ya Amnoni.

Hivyo kila mtu akatoka

"Kutoka nje kwa mtu" inamaanisha kuwaacha.

2 Samuel 13:10

Ili nile mkononi mwako

Hili ni ombi kwa Tamari kumhudumia chakula binafsi

Usinilazimishe

Hii inamaanisha kwamba "usinilazimishe kulala nawe"

Jambo lisilofaa

La kuaibisha sana

2 Samuel 13:13

Maelezo ya Jumla

Tamari anaendelea kuongea na Amnoni

Ningeenda wapi kujiepusha na aibu ambayo ingewekwa juu yangu maishani?

Tamari anauliza swali hili kusisitiza kiasi gani angeona aibu kama atalala naye.

Kujiepusha na aibu hii.

Tamari anazungumzia kuondoa aibu yake kama vile ingekuwa adui au mtesaji aliyetaka kumkwepa.

2 Samuel 13:15

Maana uovu huu wa kunifanya niondoke ni mkuu zaidi

Jina la dhahania "uovu huu mkuu" linaweza kuoneshwa kwa kitenzi.

Funga mlango nyumba yake

Hii inamaanisha kufunga mlango ili asiingie tena.

2 Samuel 13:18

Akafunga mlango nyuma yake

Hii inamaanisha kufunga mlango ili kwamba asiweze kuingia tena.

akaweka majivu kichwani pake na kuchana vazi lake. Akaweka mikono yake kichwani pake

Haya ni matendo ya kuomboleza au kuhuzunika katika utamaduni wa Kiisraeli. Hii ilionesha kwamba alikuwa na huzuni sana.

2 Samuel 13:20

Je amekuwa nawe Amnoni nduguyo?

Hii ni njia laini ya kuuliza je Amnoni amekuwa na uhusiano wa tendo la ndoa nawe.

Nyamaza

Hii inamaanisha kutomwambia mtu juu ya jambo fulani.

Usiliweke jambo hili moyoni

Kifungu "kuweka jambo moyoni" inamaanisha "kuhofu juu yake."

Hivyo Tamari akabaki peke yake

Hii inamaanisha kwamba hakuolewa.

hakusema lolote

"alinyamaza"

2 Samuel 13:23

Ikawa baada ya miaka miwili mizima

Hii inamaanisha kuwa miaka miwili imepita na inatambulisha tukio linalofuata katika habari. Kifungu "mikaa kamili" inamaanisha miaka miwili kamili.

Wakata manyoya

Hawa ni watu wanaokata manyoya ya kondoo

Baal Hazori

Hili ni jina la mahali.

Basi tazama

Hiki ni kifungu inachotumika kuonesha umakini kwa ajili ya kile kinachofuata.

mtumishi wako

Absalomu anajiita "mtumishi wako" kuonesha heshima.

Anawakatao kondoo manyoya

Ilikuwa desturi kwa watu katika Israeli kufanya sherehe baada ya kukata kondoo wao manyoya.

mfalme aweza

Japokuwa na aongea na mfalme baba yake, anamwita "mfalme" badala ya "wewe" kuonesha heshima yake.

2 Samuel 13:25

Tafadhari mwache ndugu yangu Amnoni aende nasi

Mwana mkuu alimwakilisha baba yake katika utamaduni wa Kiisraeli. Amnoni alikuwa mwana mkuu wa Daudi.

Kwa nini Amnoni aende nanyi?

Daudi alifahamu kwamba Absalomu na Amnoni hawakuwa marafiki.

2 Samuel 13:27

Absalomu alimsihi Daudi

Hapa mwandishi anamzungumzia Absalomu akimsihi Daudi kumwacha Amnoni kuja kama vile kuweka msukumu wa kimwili juu yake.

Msiogope

Hii inamaanishi hawaitaji kuogopa matokeo ya kumwua Amnoni.

Je siyo mimi niliyewaagiza?

Absalomu anauliza swali hili kusistiza kwamba atalaumiwa yeye kwa kuagiza wafanye hivyo.

si kuwaagiza

Kile alichokiagiza Absalomu kinaweza kuelezwa kwa swali kama je sikuwaagiza kumwua?

wana wote wa mfalme

Hii haiwahusishi Absalomu na Amnoni aliyekufa. Inawahusu wana wa mfalme aliowaruhusu kwenda kwenye sherehe.

kila mtu

Hii inahusisha wana wa mfalme walioondoka shereheni.

2 Samuel 13:30

Hivyo ikawa

"Ikatukia." Kifungu hiki kimetumika kutambulisha tukio linalofuata katika habari.

Njiani

"kusafiri njiani"

Habari ikamfikia Daudi kusema

Hapa inasema kwamba habari ilikuja,mtu alikuja na kumwambia Daudi ile habari.

Ndipo mfalme alipoinuka

"Kisha mfalme akainuka"

akachana nguo zake, na kulala juu ya sakafu

Alifanya hivi kuonesha kwamba alikuwa na huzuni sana.

pamoja na nguo zao zimechanwa

Walifanya hivi kuonesha huzuni yao na kuomboleza pamoja na mfalme.

2 Samuel 13:32

Yehonadabu... Shama

Huyu ni mwana wa nduguye Daudi

Bwana wau asiamini

"Bwana wangu, usiamini"

bwana wangu

Yehonadabu anamwita Daudi "bwana wangu" kuonesha heshima.

Amnoni alimwaribu dada yake

Hii ni njia rahisi ya kusema Amnoni alimbaka dada yake.

bwana wangu mfalme asi

"bwana wangu mfalme, usi"

kuweka taarifa hii moyoni

Kifungu "kuweka jambo moyoni" inamaanisha "kuhofu juu ya jambo fulani."

2 Samuel 13:34

Kuangalia

Hii inamaanisha mtumishi alikuwa akiangalia kwa mbali wakati akilinda katika ukuta wa mji.

Kuinua macho yake

Hapa mtumishi anaangalia juu ya kitu kinachozungumziwa kama aliinua macho yake.

Hivyo ikawa

Kifungu hiki inatambulisha jambo linalofuata katika habari.

Wakainua sauti zao

Hapa wana kulia kwa sauti kunasemwa kama vile sauti zao zilikuwa kitu kilichoinuliwa angani.

2 Samuel 13:37

Talmai... Amihudi

Haya ni majina ya wanaume.

kwa ajili ya mwanawe

"mwanawe Amnoni"

Alipokuwa kwa miaka mitatu

"Alipokaa kwa muda wa miaka mitatu"

Akili wa Mfalme Daudi ulitamani

Hapa Daudi anarejerewa kwa moyo wake kusisitiza mawazo yake.

Maana alikuwa amefarijika kuhusu Amnoni na kifo chake.

"Hii ni kwa sababu hakuwa na huzuni tena juu ya Amnoni kufa.

2 Samuel 14

2 Samuel 14:1

Basi

Neno hili linatumika hapa kuonesha kikomo katika habari kuu. Hapa mwandishi anazungumzia mtu mwingine katika habari.

Seruya

Hili ni jina la mwanamme

Kufahamu

Hii inamaana kuwa Yoabu alitambua alichokuwa anafikiri Daudi.

akapeleka neno Tekoa na kutaka mwanamke mwerevu aletwe.

Hii inamaanisha kuwa alituma mtu akiwa na ujumbe huko Tekoa na kumletea mwanamke.

Tekoa

Hili ni jina la eneo

Uwe kama mwanamke aliyeomboleza

Yoabu anatoa mlinganisho, akieleza kwa mwanamke jinsi alivyomtaka aonekane.

aliyekufa

Hii inarejea kwa mtu aliyekufa, siyo wafu wote kwa jumla.

2 Samuel 14:4

akainamisha uso wake juu ya ardhi

Alifanya hivyo kuonesha heshima yake na utii kwa mfalme.

mmoja alimpiga mwingine

"mmoja wa wanangu alimpiga mwenzake kwa kitu.

2 Samuel 14:7

ukoo wote

"familia yangu yote"

Mtumishi wako

Mwanamke anatumia jina hili kuonesha heshima yake kwa mfalme

Kumwua

Hii inamaanisha kuua

Wangemwaribu na mrithi pia

Ikiwa wangemwua na ndugu mkosaji kusingekuwa na mwana aliyesalia kurithi mali ya familia.

Hivyo wangelizima hata kaa liwakalo lililosalia

Hapa mwanamke anarejerea kwa mwana pekee aliyesalia kama kaa liwakalo. Anazungumzia mtu kumwua mwanawe kama kulizima kaa liwakalo.

Hawatamwachia mme wangu siyo jina wala mzao

Hii inaweza kuelezwa katika muundo chanya.

Siyo jina wala mzao

Hii inahusu mwna kubeba jina la familia kwa kizazi kijacho.

juu ya uso wa nchi

"juu ya nchi." Kifungu hiki kinasisitiza familia isingeendelea kuwepo baada ya mme kufariki. "juu ya nchi" inamaanisha juu ya ardhi ambapo watu wanatembea.

2 Samuel 14:8

Nitaagiza jambo utakalofanyiwa

Inamaanisha nitalishugulikia jambo hili

Tekoa

Ni jina la sehemu

Hatia iwe juu yangu na juu ya familia ya babangu

Hii inamaanisha kwamba ikiwa watu watasema kwamba mfalme amekosea kusaidia familia ya mwanamke yeye hatakuwa na hatia.

mfalme na kiti chake cha enzi

Hapa neno "kiti cha enzi" linarejerea yeyote angekuja kuwa mfalme mahala pa Daudi.

Hawana hatia

"Ni msafi." Hapa mwanamke anaongelea mfalme kuwa safi kwa kuisaidia familia yake ikiwa angekuwa ameisaidia tayari.

2 Samuel 14:10

Kusema chochote kwako

Hapa vitisho vya maneno vinazungumzwa kwa ujumla.

Hatakugusa tena

Hapa Daudi anazungumzia mtu kutomgusa au kumtisha, kwa kusema kwamba mtu hata kugusa. Inaonesha kwamba Daudi hataruhusu mtu kumtisha ili kumsumbua.

kwamba wasimwaribu mwanangu

"Kwamba hawatamwua mwanangu" au "kwamba hawatamnyonga mwanangu"

Tafadhari, mfalme na amkumbuke Yahwe Mungu wake

Maana kisiwa 1) Kifungu "kukumbuka" ni usemi unaomaanisha kuomba. Yaani "Tafadhari mwombe Yahwe Mungu wako au 2) Hapa "kumbuka" inamaanisha kukumbuka na inaonesha kwamba baada ya kumkumbuka Yahwe atatoa ahadi kwa jina lake.

Mlipa kisasi cha damu

Hii inarejerea kwa mtu anayetaka kulipiza kisasi cha kifo cha ndugu yake.

Kumwangamiza mwingine zaidi

"kusababisha mwingine zaidi afe." Hii ni nyongeza kwa mwingine aliyeuawa.

Hakuna hata unywele mmoja wa mwanao utakaoanguka chini.

Hii inamaana kwamba mwanawe hatapata madhara, ambayo inatia chumvi kwamba hatapoteza hata unywele mmoja.

Kama Yahwe aishivyo

Mara kwa mara watu waliahidi na kulinganisha kwa uhakika jinsi ambavyo wangeakikisha ahadi zao kwa jinsi Yahwe anavyoishi.

2 Samuel 14:12

sema neno zaidi

"kusema nawe neno zaidi." Mwanamke anaomba kusema na mfalme jambo lingine.

Mtumishi wako

Kuonesha heshima kwa mfalme

Kuongea zaidi

Mfalme alimpa ruhusu kuongea zaidi.

Kwa nini basi umetenda jambo la namna hiyo kwa watu wa Mungu?

Mwanamke anauliza swali hili kumkemea Daudi kwa jinsi alivyomtendea Absalomu.

Mfalme ni kama mwenye hatia

Mwanamke anamlinganisha mfalme na mtu mwingine aliye na hatia bila kusema moja kwa moja.

Mwanawe aliyefukuzwa

Hii inaweza kuelezwa kama "mwanawe aliyetengwa.

Maana wote ni lazima tufe, nasi ni kama maji tukimwagika juu ya ardhi... juu tena.

Hapa mwanamke anazungumzia mtu anayekufa kama maji yamwagikayo juu ya nchi.

Mungu... hutafuta njia kwa wale waliofukuzwa kurudishwa tena.

Mwanamke anaonesha kwamba Daudi anapaswa kumrudisha mwanawe.

2 Samuel 14:15

kwa sababu watu wamenitisha.

Maneno yanayokosekana yanaweza kuongezwa katika kifungu hiki. Yaani "kwa sababu watu wameniogopesha hata nimekuja"

Mtumishi wako

Hii ni kuonesha heshima kwa mfalme hivyo anajiita "mtumishi wako"

Kumtoa mtumishi wake

Hapa kifungu "kumtoa" inamaanisha kumkabizi katika mikono ya mtu mwingine.

Kutoka katika mkono wa mtu

Hapa "mkono" unarejerea katika mamlka ya mtu.

Kutoka katika urithi wa Mungu

Hii inamaanisha kwamba wasingekuwa na mzao yeyote wa kuishi katika nchi ambayo ingelithiwa na wazao wao.

Neno la bwana wangu mfalme

Kirai jina "neno" kinaweza kuelezwa na kitenzi "husema"

Maana kama malaika wa Mungu, ndivyo alivyo bwana wangu... kutoka uovu

Hapa Daudi, mfalme, analinganishwa na "malaika wa Mungu." Hii ni kwa sababu wote wanajua jinsi ya kutofautisha mema kutoka mabaya.

2 Samuel 14:18

Tafadhari usinifiche neno lolote nikuulizalo

Muundo wa kinyume umetumika hapa ili kusisitiza na unaweza kuelelezwa kwa muundo chanya. Yaani "tafadhari niambie ukweli kuhusu lolote ninalokuuliza"

Je si mkono wa Yoabu uliopamoja nawe katika hili

Hapa neno "mkono" linaonesha ushawishi wa Yoabu.

Kama uishivyo

"Hakika kama uishivyo." Hapa mwanamke analinganisha uhakika wa alichokisema Daudi amesema kwa hakika kwamba anaishi, ili kusisitiza jinsi taarifa ilivyo ya kweli

Hakuna awezaye kuelekea mkono wa kulia... mfalme alivyosema

Hapa mwanamke anaeleza ugumu wa kuongea na mfalme na kumficha asigundue ukweli kwa kulinganisha na mtu asivyoweza kuelekea upande wowote.

Mkono wa kulia au wa kushoto

Taarifa inatoa milengo miwili na inamaanisha "popote."

Bwana wangu ni mwelevu

Bwana wangu mfalme ni mwenye hekima"

Ni mwenye hekima, kama hekima ya malaika wa Mungu

Mwanamke analinganisha hekima ya Daudi na ya malaika kusisitiza jinsi alivyo mwenye hekima.

2 Samuel 14:21

Hivyo mfalme akamwambia Yoabu

Hii inamaana kwamba mfalme alitaka Yoabu aletwe mbele yake ili kwamba aongee naye.

Basi tazama

Kifungu kimetumika kuonesha usikivu wa mtu kwa kusikiliza kwa makini kinachosemwa baada ya hapo.

Jambo hili

Hii inarejea kwa anachotaka Yoabu mfalme akifanye.

Yoabu akainamisha uso wake chini

Yoabu alifanya hivi kwa kumweshimu mfalme na kuonesha shukurani yake.

mtumishi wako

Hii ni kuonesha heshima kwa mfalme

Nimepata kibari mbele zako

Kifungu "kuona kibari" kinamaanisha kuthibitishwa na mtu fulani. Kifungu "mbele yako" kinarejea kwa anachokifikiri mfalme.

Katika hilo mfalme

"kwa sababu mfalme"

Mfalme ametimiza haja

"Umefanya nilichokuomba kufanya"

2 Samuel 14:23

lakini hataweza kuuona uso wangu... uso wa mfalme

Hapa neno "uso" linamrejerea mfalme.

2 Samuel 14:25

Basi

"Basi" inaonesha badiliko katika habari kuu. Hapa Samweli anatoa sehemu nyingine ya habari.

Hakukuwa na mtu katika Israeli aliyesifiwa kwa uzuri kama Absalomu

Watu walimsifu Absalomu kwa uzuri wake wa sura kuliko walivyomsifu mwingine yeyote.

Kutoka katika wayo wa mguu wake hadi katika utosi wake hakuwa na waa lolote

Hii inamaanisha kwamba hakuwa na kasoro.

shekeli mia mbili

Katika vipimo vya sasa ni sawa na "kilo mbili na nusu"

Kwa kiwango cha kipimo cha mfalme

Mfalme alikuwa na kipimo kilichoamua kiwango cha uzito wa shekeli, uzito mwingine na vipimo vingine.

Walizaliwa kwa Absalomu wana watatu na binti mmoja

Inamaanisha Absalomu alikuwa na watoto watatu wa kiume na binti mmoja.

2 Samuel 14:28

Uso wa mfalme

Hii inamaansisha mfalme.

Absalomu akatuma neno kwa Yoabu

Hii inamaanisha kwamba alittuma mjumbe kwa Yoabu akiwa na ombi.

Kumpeleka kwa mfalme

Inaoneshwa kwamba Absalomu alimtaka Yoabu kuja kwake ili amwone na kuingilia kati ili aweze kumwona mfalme.

Hivyo Absalomu akatuma neno mara ya pili

Hii inamaanisha kwamba alituma tena mjumbe kwa Yoabu akiwa na ombi lilelile.

2 Samuel 14:30

Tazama

Hapa neno hili linatumima kama usemi kuwakumbusha watu juu ya jambo fulani.

2 Samuel 14:32

Tazama

Neno hili limetumika hapa kama usemi kusisitiza, na kuthibitisha kinachosemwa baada ya hapa.

Nilituma neno

Hii inamaana alituma mjumbe.

Kwa mfalme kusema

Ujumbe kwa mfalme hapa umeandikwa kama Absalomu ndiye alikuwa mzungumzaji. Absalomu alikuwa akimwomba Yoabu kusema ujumbe kwa niaba yake.

Uso wa mfalme

Hii inamrejerea mfalme.

Aliinama chini mbele ya mfalme hadi kwenye ardhi

Absalomu anaonesha heshima kwa mfalme.

Mfalme akambusu Absalomu

Hii inamaanisha kwamba mfalme alisamehe na kumrudisha Absalomu.

2 Samuel 15

2 Samuel 15:1

Ikawa

Kifungu hiki kinatambulisha tukio jingine katika habari

Na watu hamsini kwenda mbele yake

Watu hawa wangekwenda mbele ya kibandawazi kwa kumweshimu Absalomu.

Mtumishi wako

Mtu alipomjibu Absalomu alimrejerea kwa kusema "mtumishi wako" kuonesha heshima yake kwa Absalomu.

2 Samuel 15:3

Hivyo Absalomu angemwambia

Inaonesha kwamba mtu alimwambia Absalomu shitaka lake. Yaani Absalomu angemwuliza tatizo lake lilikuwa ni nini, ndipo mtu alipomweleza Absalomu kwa nini alitafuta haki.

Vema na haki

Maneno yana maana moja na yanatumika pamoja kusisitiza kwamba shitaka lake lilikuwa jema.

kusikiliza kesi yako

"Kusikiliza" shitaka inamaanisha kuisikiliza na kufanya maamuzi.

2 Samuel 15:5

yeye hunyosha mkono na kumshika na kumbusu

Hili ni tendo la salamu ya kiurafiki.

kwa hukumu

Hii inamaanisha kwamba walimjia mfalme ili kuamua migogoro yao

Hivyo Absalomu akaiba mioyo ya watu wa Israeli

Hii inamaanisha kwamba Absalomu aliwashawishi watu kumtii yeya zaidi ya Daudi. Hapa mwandishi anaongelea jinsi watu walivyomtii Absalomu kwa kusema aliiba mioyo ya watu.

2 Samuel 15:7

Ikawa

Kifungu hiki kinatumika kutambulisha tukio linalofuata katika habari.

hata mwisho wa miaka minne Absalomu

Hii inarejerea miaka minne baada ya kurudi Yerusalemu.

na kutimiza nadhiri niliyoiweka kwa Yahwe nilipokuwepo Hebroni

"kwenda Hebroni na pale nitatimiza nadhiri niliyomfanyia Yahwe"

Kwa miaka minne

Hapa Absalomu anajirejerea katika namna ya kumweshimu mfalme.

2 Samuel 15:9

Hivyo Absalomu akainuka

"Hivyo Absalomu anaondoka"

Katika makabila yote ya Israeli

Hapa sehemu walipoishi makabila ya Israeli zinatajwa kama makabila yenyewe.

Sauti ya tarumbeta

"tarumbeta ikipigwa"

2 Samuel 15:11

Waliokuwa wamearikwa

Inamaanisha "watu waliokuwa wamepewa taarifa"

Wakaenda katika ujinga wao

Hawakuwa wanatambua kwa undani kilichokuwa kinakwenda kutendeka

Akamwita Ahithofeli

Hii inamaanisha kwamba alituma wajumbe kumwita Ahithofeli na kumleta kwake.

Ahithofeli

Hili ni jina la mwanamme.

Gilo

Hili ni jina la sehemu.

2 Samuel 15:13

Mioyo ya watu wa Israeli inaambatana

Hapa watu wanarejerewa kwa "mioyo" kusisitiza utiifu wao kwa Absalomu.

kujiepusha na Absalomu... kwa haraka... na ataleta

Hapa Daudi anaongelea Absalomu na watu aliokuwa nao kama "Absalomu" yeye mwenyewe kwa sababu watu walikuwa wanafuata mamlaka ya Absalomu.

kuushambulia mji kwa ukali wa upanga

"Mji" unatajwa kuonesha watu wa mji. "Ncha ya upanga" inarejerea kwa panga za waisraeli kusisitiza kwamba waliwaua watu vitani.

kusababisha madhara

Hii inamaanisha kusababisha madhara kutokea.

2 Samuel 15:16

kulitunza kasiri

Hapa neno "kutunza" linamaanisha kutunza.

katika nyumba ya mwisho

Hii inarejerea nyumba ya mwisho ambayo wangefikia wakati wanaondoka mjini.

Wakerethi... Wapelethi

Hawa walikuwa watumishi wa Daudi

Wagiti

Hili ni kundi la watu waliokuwa katika nchi ya Palesitina

Watu mia sita

"watu 600"

2 Samuel 15:19

Itai

Hili ni jina la mwanamme.

Mgiti

Hii ni aina ya kabila fulani

Kwa nini ulikwenda nasi pia?

Swali hili linaonesha kwamba mfalme hakuwa amewaomba kwenda naye.

Kwa nini mimi niwafanye mtangetange pamoja nasi?

Swali hili linasisitiza kwamba Daudi hakutaka Itai aende.

Kwa vile uliondoka jana tu

Kutia chumvi huku kunatumika kusisitiza. Itai Mgiti alikuwa amekaa pale kwa miaka kazaa.

Utiifu na uaminifu na uambatane nanyi.

Hii ni baraka ambayo Daudi anampa.

2 Samuel 15:21

Kama Yahwe aishivyo, na kama bwana wangu mfalme aishivyo

Hapa mwandisha anafanya ahadi ya dhadi. Analinganisha uhakika wa kutimiza ahadi kwa uhakika wa kuishi kwa mfalme na Yahwe.

mtumishi wako

Itai anajitaja kwa heshima ya mfalme.

kwamba ni maisha au kifo

"hata kama nitauawa nikikusaidia"

Nchi yote ikalia kwa sauti kuu

Wengi wa watu wa Israeli walilia kwa sauti walipomwona mfalme akiondoka. Huku ni kutia chumvi kwamba nchi yote ililia.

kwa sauti kuu

Hapa watu wengi waliokuwa wakilia wanatajwa kama walishirikiana sauti kuu.

Bonde la Kidroni

Hili ni jina la eneo karibu na Yerusalemu

2 Samuel 15:24

Nikiona kibari machoni pa Yahwe

Hapa "macho ya Yahwe" inaonesha mawazo na maoni ya Yahwe. Ikiwa "nitaona kibari" inamaanisha kama atapendezwa nawe.

Mahali aishipo

"Mahali uwepo wake ulipo." Sanduku la agano linaashiria uwepo wa Yahwe. Hii inarejerea mahali sanduku lilipo.

2 Samuel 15:27

Ahimaasi

Hili ni jina la mwanamme.

Abiathari

Hili ni jina la mwanamme

Je wewe si mwonaji?

Swali hili linatumika kumkemea Sadoki.

Tazama

Hii inamtaka msikilizaji kuwa msikivu kwa kinachofuata.

Hata neno litakapotoka kwenu

Hii inaonesha yeye akipeleka mjumbe kwa mfalme.

Kunitaarifu

Hapa mfalme anaonesha kwamba atapokea ujumbe kumtaarifu kinachofanyika Yerusalemu.

2 Samuel 15:30

mikuu mitupu

bila kuvaa viatu au kandambili

kichwa chake kimefunikwa

Hii ni ishara ya kuomboleza na aibi

Ahithofeli

Hili ni jina la mwanamme

waaini

Watu wanaoungana kinyume cha mwingine

Tafadhari ligeuze shauri la Ahithofeli katika upumbavu

Daudi anamwomba Yahwe alifanye shauri la Aithofeli katika upumbavu na kutokufaa.

2 Samuel 15:32

Ikawa

"Ilitukia." Kifungu hiki kinaonesha tukio linalofuata katika habari.

juu njiani

Neno "juu" limetumika hapa kwa sababu Daudi alipanda juu katika mwinuko na yupo juu ya kilima.

Mahali Mungu alipokuwa akiabudiwa

Hii inaweza kuelezwa kuwa "mahali ambapo watu walikuwa wakimwabudu Mungu"

Hushai

Hili ni jina la mwanamme.

Mwarki

Hili ni jina la kundi la watu.

Vazi lake likiwa limechanwa na udongo kichwani

Hili ni tendo la kuonesha aibu au toba. Hapa neno "udongo" linamaanisha uchafu.

Utalibadili shauri la Aithofeli kwa ajili yangu

Maoni ya Daudi kwa Hushai kwamba apinge kile Aithofeli anachoshauri.

2 Samuel 15:35

Je haunao pamoja nawe Sadoki na Abiathari makuhani?

Daudi anauliza swali hili ili kumwambia Hushai kwamba hayupo peke yake. Yaani kuonesha kwamba "Sadoki na Abiathari makuhani watakuwepo kukusaidia."

chochote unachosikia... lolote usikialo

Hii ni kuzidisha maana; haimaanishi kila neno asikialo. Inamaanisha mambo muhimu ayasikiayo.

Ahimaasi... Yonathani

Haya ni majina ya watu.

Kwa mikono yao

Kifungu "mikono yao" kinarejerea kwa wana na kinamaanisha kwamba wangehudumu kama wajumbe.

2 Samuel 16

2 Samuel 16:1

Siba

Hili ni jina la mwanamme

Mefiboshethi

Hili ni jina la kijana wa Yonathani mwana wa Sauli.

Mikate mia mbili... vichala mia moja... vishada mia moja

"mikate 200 ... vichala 100... vishada 100"

Vipande vya mikate

visehemu vya mikate

vishada mia moja vya mizeituni... vishada vya tini

Kifungu hiki kinamaanisha vishada vya mizeituni vilivyosindikwa pamoja

Mizeituni

vichala vilivyo kaushwa

Kiriba vya mvinyo

"Kiriba cha ngozi kilichojaa mvinyo"

Kuzimia

"Kuchoka sana sana"

2 Samuel 16:3

Mjukuu wa bwana wako

"Mefiboshethi, mjukuu wa bwana wako"

mjukuu

mwana wa mtoto wa mtu.

Tazama

Hapa neno hili linatumika kuvuta makini ya mtu kwa kinachofuata.

Nyumba ya Israeli

Hii inahusu watu wa Israeli

Nitaurudisha ufalme wa baba yangu kwangu

Mjukuu wa Sauli kuruhusiwa kutawala kunazungumzwa kana kwamba ni kuurudisha ufalme katika familia yao.

Mefiboshethi

Hili ni jina la mwanamme, aliyekuwa kijana wa Yonathani mwana wa mfalme Sauli.

Nainama kwa unyenyekevu kwako

Siba hainami kiuhalisia mbele za mfalme anapoongea. Hii inamaanisha kwamba atamtumikia mfalme kwa kiwango kilekile cha unyenyekevu kama ambavyo angefanya kama angeinama kiuhalisia mbele zake.

kupata kibari mbele zako

Kifungu "kuona kibari" kinamaanisha kukubaliwa na mtu. Kingungu "mbele zako" inaonesha anachofikiri mfalme.

2 Samuel 16:5

Bahurimu

Jina la mahali

Shimei... Gera

Haya ni majina ya wanaume

Badala ya

"Hata hivyo kulikuwa na"

Walinzi

Hawa ni watu wanaomlinda mtu mhimu.

2 Samuel 16:7

mwovu

Mtu mwovu, mkosaji au mvunja sheria.

mtu wa damu

Hapa "damu" inaonesha watu wote aliokuwa amewaua vitani.

Yahwe amekulipa

Yahwe anawalipa kwa kuwaadhibu.

Kwa damu ya familia ya Sauli

Hapa "damu" inaonesha watu waliokuwa wameuawa kutoka katika familia ya Sauli. Mfalme alikuwa anawajibika kwa kufa kwao.

ambaye umemiliki badala yake

Daudi alitawala kama mfalme juu ya watu ambao Sauli alikuwa amewamilki.

katika mkono wa Absalomu

Hapa "mkono" unaonesha mamlaka.

2 Samuel 16:9

Abishai

Hili ni jina la mwanamme

Seruya

Hili ni jina la mwanamme

Kwa nini mbwa mfu huyu amlaani bwana wangu mfalme

Abishai aliuliza swali hili kuonesha hasira yake juu ya mtu yule.

Umbwa mfu huyu

Hapa mtu anaelezwa kwamba hafai kwa kulinganishwa na mbwa mfu.

Nifanye nini nanyi, wana wa Seruya

Swali hili liliulizwa ili kuwakosoa wana wa Seruya.

Pengine ananilaani kwa sababu

"Anaweza kuwa ananilaani kwa sababu"

Mlaani Daudi.' Nani sasa awezaye kumwambia, 'Kwa nini unamlaani mfalme

Hii inasemwa kama swali kusisitiza kwamba jibu ni kwamba "hakuna."

2 Samuel 16:11

Mwanangu, aliyetoka katika mwili wangu

Daudi anamweleza mwanawe katika njia hii kusisitiza ukaribu uliopo kati ya baba na mwana.

anataka kuchukua uhai wangu

Hii ni njia laini ya kuonesha hali ya kumwua mtu.

Si zaidi sana mbenjamini huyu akatamani anguko langu

Daudi anatumia swali hili kuonesha kwamba hashangazwi kwamba mtu yule anataka kumwua.

anatamani anguko langu

Hapa Daudi anaelezea tamaa ya mtu ya kumwua kama vile Daudi alikuwa kitu ambacho mtu alitaka kukiangamiza.

Mwache peke yake alaani

Hapa kifungu "mwache peke yake" kinamaanisha kuacha kumzuia kufanya anachokifanya.

ataangalia

Hapa "kutazama" kunamaanisha "kujari"

maangaiko niliyofungiwa

Hapa Daudi anazungumzia maangaiko kama vile yalikuwa ni mnyama mkari ambaye Mbenjamini amemfungia.

2 Samuel 16:13

Shimei alikwenda kando yake juu ya upande wa kilima

Shimei alikuwa akitembea sambaba na Daudi na watu wake, japokuwa Shimei alikuwa juu upande wa kilima.

2 Samuel 16:15

Ahithofeli

Hili ni jina la mwanamme

Hushai

Hili ni jina la mwanamme

Ikawa kwamba

"Ikawa kwamba." Kifungu hiki kinatumika kutambulisha tukio linalofuata katika habari

Mwarki

Hili ni jina la mwanamme

2 Samuel 16:17

Utiifu

Hisia nzito ya kusaidia na upendo

Je huu ndiyo utiifu wako kwa rafiki yako? Kwa nini haukwenda pamoja naye?

Maswali haya yanaulizwa kumkosoa Hushai.

Yule ambaye Yahwe

Hushai anamrejerea Absalomu

Yule ambaye... huyo ndiye mtu... pamoja naye

Hapa Hushai anamrejerea Absalomu katika nafsi ya tatu kuchukua msisitizo kutoka kwake na kuelekeza kwa Yahwe na watu aliowachagua. Hii inaweza kuandikwa katika nafsi ya pili.

2 Samuel 16:19

Kwani ni nani ninayepaswa kumtumikia? Je sipaswi kutumika mbele za mwana?

Hushai anauliza swali hili kusisitiza kwamba anataka kumtumikia Absalomu.

2 Samuel 16:20

Ahithofeli

Hili ni jina la mwanamme

kulitunza kasiri

Kifungu "kutunza" kinamaanisha kuangalia.

kuwa kitu kinachonuka mbele ya baba yako

Ahithofeli anazungumia Absalomu kumchukiza baba yake kama vile kingekuwa kitu ambacho kina harufu ya kuchukiza.

Kisha mikono ya wote walio pamoja nawe itatiwa nguvu

Hapa watu waliomfuata Absalomu wanarejerea kwa kutaja mikono yao. Habari hii itaitia nguvu utiifu wa watu kwa Absalomu na kuwapa hamasa.

2 Samuel 16:22

Kutanda

"Kuweka"

juu ya kasri na Absalomu akalala... masuria wa baba yake mbele za Israeli wote.

Hii inamaanisha kwamba watu walikuwa wanaweza kuliona hema na Absalomu akiingia na kutoka ndani ya hema pamoja na wanawake. Kifungu hiki "Israeli wote" kinatia chumvi, maana ni wale tu walikuwa karibu na kasiri wangeweza kuiona.

Basi ushauri wa Ahithofeli... ilikuwa kama vile mtu alisikia

Hapa mwandishi analinganisha ni kwa kiasi gani watu waliamini ushauri wa Ahithofeli kama vile ambavyo wangeamini ushauri wa moja kwa moja kutoka kwa Mungu.

kama mtu anavyosikia kutoka katika kinywa cha Mungu mwenyewe

Hapa kinywa cha Mungu kinamwakilisha na kinasisitiza hotuba yake.

2 Samuel 17

2 Samuel 17:1

Ahithofeli

Hili ni jina la mwanamke

Watu kumi na mbili elfu

"watu 12,000"

inuka na

"kuanza ku"

njoo

"Kuja kwa"

amechoka na dhaifu

Kimsingi maneno haya yanamaanisha kitu kimoja na yanatumika kwa pamoja kusisitiza jinsi Daudi alivyokuwa dhaifu.

tutamshangaza kwa hofu

Hapa neno "hofu" laweza kuelezwa kwa kisifa "kuogopa."

Nitamshambulia mfalme peke yake

Inaonesha kwamba alikusudia kumwua mfalme.

kuwarudisha watu wote

Hii inamaanisha watu wote waliokuwa pamoja na Daudi.

kama bibi harusi akija kwa mmewe

Hapa Ahithofeli anazunguza furaha ya watu kwa kulinganisha na furaha ya bibi harusi.

Kuwa katika amani

Hii inamaanisha kuwa na amani au kuishi kwa amani.

chini yako

Hii inahusu kuwa chini ya mamlaka ya mfalme.

2 Samuel 17:5

Hushai Mwarki

Huyu alikuwa rafiki wa Daudi

Ahithofeli

Hili ni jina la mwanaume.

2 Samuel 17:8

Wako kama dubu aliyenyang'anywa watoto wake

Hasira ya askari hapa inalinganiswa na dubu jike aliyenyang'anywa watoto wake.

dubu

mnyama mkubwa na mkali anayetembea kwa miguu minne na ana makucha na meno makali

Mtu wa vita

Hii inamaanisha amepigana vita nyingi na anajua kwa kina njia ya vita.

Tazama

Neno hili limetumika kuvuta makini ya mtu kwa kile kinachofuata

shimo

tundu refu katika ardhi

au katika sehemu ningine

Hili ni eneo lingine analoweza kuwa amejificha.

baadhi ya watu wako watakapokuwa wameuawa

Inamaanisha watu wa Daudi watakapokuwa wamewauwa baadhi ya watu wa Absalomu

mauaji yamefanyika kwa askari wanaomfuata Absalomu

Nomino "machinjo" inamaanisha tukio ambapo watu wengi wameuawa kwa ukatili.

ambao mioyo yao ni kama mioyo ya simba

Hapa askari wanatajwa kwa "mioyo" yao. Pia, ujasiri wao mkuu unalinganishwa na ule wa simba.

2 Samuel 17:11

kwamba Israeli wote wakusanywe pamoja kwako

Askari wote wanatajwa hapa kama "Israeli wote"

kutoka Dani hadi Beersheba

Kifungu hiki kinamaanisha kutoka mpaka wa kaskazini hadi mpaka wa kusini wa Israeli

wengi kama mchanga ulioko ufuweni mwa bahari

Hii ni kuzidisha maana pale chembe zote za mchanga zinalinganishwa na idadi ya askari wa Israeli.

kwamba wewe mwenyewe unakwenda vitani

Kifungu hiki "binafsi" kinamaanisha kwenda wewe mwenyewe na wala siyo kutuma mtu mwingine.

kuja juu yake

Hii inamaana ya kwenda kwake kwa kusudi la kumshambulia.

tutamfunika kama umande unavyofunika ardhi

Jeshi la Absalomu linaelezwa kulifunika jeshi la Daudi kama umande unavyoifunika ardhi wakati wa asubuhi.

umande

mvuke unaoanguka juu ya ardhi kama maji na kuifunika ardhi wakati wa usiku na kuacha ardhi imeloa.

Hatutaacha hata mmojawao ... akiwa hai

Sentensi hii imetumika kusisitiza kwamba watamwua kila mtu.

Yeye mwenyewe

Maneno haya yote yanamtaja Daudi.

2 Samuel 17:13

Ndipo Israeli wote

Hii inawahusu askari wa Israeli na siyo Waisraeli wote.

tutaleta kamba juu ya mji huo na kuukokotea mtoni, hata kusionekane hata jiwe moja dogo lililosalia

Hii inamaanisha kwamba askari wangeuangusha mji chini na kukokota vipande vyake katika mto

hata kusionekane hata jiwe moja dogo lililosalia.

Hii ni kutia chumvi kwa kueleza ni jinsi gani watakavyouangamiza mji. Hii siyo katika hali halisia.

Hushai Mwarki

Huyu ni rafiki wa mfalme Daudi. Arki ni jina la kundi la watu katika Israeli

Ahithofeli

hili ni jina la mshauri wa Daudi

Kukataliwa kwa shauri jema la Ahithofeli

Neno "kukataliwa" linaweza kuelezwa na kitenzi "kataa"

kulete angamizo juu ya Absalomu

"Kuleta" kitu fulani juu ya mtu inamaanisha kusababisha jambo kufanyika kwake.

2 Samuel 17:15

Sadoki ... Abiathari

Haya ni majina ya wanaume

vile na kwa njia hiyo

Kifungu kinamaanisha "kama hivi" kuhusu kile Ahithofeli alichokuwa amekisema mwanzo

vivuko vya Araba

Hii ni sehemu ya mto isiyo na kina kirefu ambayo watu wanaweza kuvuka kwa kutembea. Araba ni nchi kandokando ya sehemu zote mbili za mto Yordani

Kwa jinsi yoyote

Hii inamaanisha kuhakikisha unafanya jambo kwa namna yoyote.

Mfalme atamwezwa

Hapa mfalme na watu wake kuuawa wanaelezwa kama vile walikuwa "wamemezwa" na adui.

2 Samuel 17:17

Yonathani... Ahimaasi

Haya ni majina ya wanaume

Ujumbe ulipokuja

Hapa "ujumbe" unaelezwa kama unakuja kwao, wakati uhalisia ni mwanamke aliyeleta taarifa kwo.

wakati huu

wakati mmoja

Hivyo Yonathani na Ahimaasi wakaondoka

Inaoneshwa kwamba walikuta kwamba kijana amemwambia Absalomu kuwepo kwao pale.

chemichemi za En Rogeli... Bahurimu

Haya ni majina ya sehemu, karibu na Yerusalemu. Bahurimu ni mji mdogo.

Wakashuka

"Waliteremka wenyewe kisimani na kujificha"

2 Samuel 17:19

Mama wa nyumba ile

"mke wa mtu yule"

Ahimaasi... Yonathani

Haya ni majina ya wanaume.

2 Samuel 17:21

Ikawa

"Ikatukia." Kifungu hiki kinaonesha tukio jingine katika habari

vuka juu ya maji haraka

Hapa "maji" yanarejerea Mto Yordani.

Ahithofeli ametoa mashauri haya na haya

usemi "haya na haya" umetumika mahali pa habari ambayo tiyari msomaji anaifahamu. Hapa inahusu ushauri alioutoa Aithofeli kwa Absalomu katika 17:1.

Hata ilipofika alfajiri hakuna hata mmoja aliyesalia kwa kutouvuka Yordani

Sentence hii imetumika kusisitiza kwamba wote walivuka mto.

2 Samuel 17:23

Ona

"jua" au "tambua"

ushauri wake haukufuatwa

Hii inaweza kuelezwa kwamb "Absalomu hakuwa ameufuata ushauri wake"

kupanda juu ya punda

Kuweka nguo au ngozi ya kukalia juu ya punda au farasi kwa aliyempanda kukaa juu yake.

Kuweka mambo yake katika utaratibu

Alijiandaa kwa kifo chake kwa kuwaambia familia yake cha kufanya baada kufa kwake.

Kwa njia hii

"Hivi ndivyo ilivyo"

alizikwa

Hii yaweza kuelezwa "kuwa walimzika"

2 Samuel 17:24

Mahanaimu... Gileadi

Hii ni baadhi ya miji katika Israeli

Amasa... Yoabu... Yetheri... Nahashi

Haya ni majina ya wanaume

Mwishimaeli

Huyu ni uzao wa Ishmaeli. Baadhi ya nakala zinaonesha kuwa "Mwisraeli"

Abigaili... Seruya

Haya ni majina ya wanawake.

2 Samuel 17:27

Ikawa

Kifungu kinatambulisha tukio linalofuata katika habari

Mahanaimu... Raba... Lo Debari... Rogelimu

Haya ni majina ya miji au sehemu.

Shobi... Nahashi... Makiri... Amieli... Barzilai

Haya ni majina ya wanaume.

Mwamoni... Mgileadi

Haya ni majina ya makundi ya watu

magodoro na mabulangeti

godoro ni kitu laini cha kulalia, na blangeti ni nguo ya kujifunika ili kupata joto.

Unga

Unga ni nafaka iliyopondwa kuwa laini na unatumika kutengeneza mkate au ugali.

Iliyookwa

"Iliyopikwa"

Maharage

mbegu zipikwazo kwa kuliwa

dengu

Ni aina ya mbegu zinazopikwa na kuliwa

siagi

maziwa yaliyoganda na kuwa magumu

Kiu

Hitaji la maji ya kunywa au kimiminika kingine.

2 Samuel 18

2 Samuel 18:1

Daudi akawahesabu askari waliokuwa pamoja naye na akaweka

Daudi hakuhesabu watu wote mwenyewe, lakini ni watu wake waliowahesabu.

Makapteni

Kapteni ni mtu mwenye mamlaka juu ya kundi la askari.

moja ya tatu... tatu nyingine

tatu... tatu nyingine - "moja ya tatu ya jeshi... therusi nyingine ya jeshi." Therusi ni sehemu moja kati ya sehemu tatu ya kitu kimoja kizima.

Abishai... Seruya

Haya ni majina ya wanaume

Itai

Hili ni jina la mwanamme.

Mgiti

Huyu ni mtu kutoka Gathi, mji wa Wafilisiti.

Mimi mwenyewe nitakwenda pamoja nanyi pia bila shaka

Hii ni kwenda pamoja na jeshi vitani.

2 Samuel 18:3

Nusu yetu

Neno "nusu" linarejea kwa kitu kimoja kati ya viwili vinavyolingana.

Wewe ni zaidi ya watu elfu kumi kati yetu

Hii inamaanisha kwamba jeshi la adui linahesabu kumwua Daudi kuna thamani ya kuua watu 10,000. Idadi ya watu 10,000 ni hesabu iliyotiwa chumvi ili kusisitiza idadi kubwa zaidi ya watu.

elfu kumi

"10,000"

Kwa hiyo ni afadhari zaidi ukitusaidia ukiwa mjini

Daudi angeweza kuwasaidia akiwa mjini kwa kuwashauri na kupeleka watu kuwasaidia.

2 Samuel 18:5

Abishai

Hili ni jina la mwanamme

Itai

Hili ni jina la mwanamme

Mmtendee kwa upole kwa ajili yangu

"Kwa ajili yangu, msimdhuru." Kifungu "mmtendee kwa upole" inamaanisha kuwa mpole kwa mtu bila kumdhuru.

Kwa ajili yangu

"faida yangu" au "kwa ajili yangu"

kijana, pamoja na Absalom

"Kijana Absalomu"

2 Samuel 18:6

jeshi likaenda nyikani dhidi ya Israel

Hii inamaanisha kwamba walikwenda na kupigana nao vitani.

eshi la Israeli likashindwa mbele ya askari wa Daudi

Inaweza kuelezwa katika muundo tendaji yaani "Askari wa Daudi walilishinda jeshi la Israeli"

Machinjo makuu

Tukio ambapo watu wengi waliuawa kwa ukatili.

Watu elfu ishirini

"20,000"

watu wengi wakaangamizwa na msitu kuliko upanga

Hapa "msitu" unaelezwa kama ulikuwa hai kuweza kufanya kitendo. "Upanga" inahusu jeshi la Daudi lililoweza kupigana kwa upanga.

2 Samuel 18:9

Ikatukia kwamba Absalomu akakutana na askari wa Daudi

Hili ni tukio lilotokea wakati wa vita.

na kichwa chake kikanaswa katika matawi ya mti

Absalomu alikuwa na nywele ndefu zilizonasa kwenye matawi ya mti.

Tazama

Neno hili linavuta makini ya mtu kwa ajili ya kinachofuata.

Ning'inia

Kuelea juu bila kukanyaga juu ya nchi au kitu.

kati ya nchi na anga

"Hewani"

Kwa nini haukumpiga hata chini

Swali hili linamaanisha alipaswa kuwa amemuua.

shekeli kumi za fedha na mkanda

Katika viwango vya sasa ni sawa na gramu 110 za fedha.

mkanda

Huu ni mkanda maalumu unaoonesha kwamba mtu fulani ni askari mwenye cheo ili apewe heshima.

2 Samuel 18:12

shekeli elfu za fedha

"shekeli 1,000 za fedha." Katika vipimo vya sasa ni sawa na salafu 1,000" au "kilo 11 za sarafu"

nisingeinua mkono wangu juu ya mwana wa mfalme

Kifungu "kuinua mkono" kinamaana ya kushambulia.

Mtu asimguse

Hapa "kugusa" inamaanisha "kudhuru"

Uongo

Neno "uongo" laweza kuelezwa kwa kirai kitenzi. Lakini pia inahusu kutotii agizo la mfalme.

Hakuna cha kufichika kwa mfalme

Hii inamaana jinsi mfalme anavyojua karibu kila kitu kitendekacho kama vile kila kitu kilikuwa na umbo kujua kilipo.

2 Samuel 18:14

Sitakusubiri

Yoabu anamaanisha kwamba hawezi kusubiri kwa kuongea na yule mtu.

Moyo wa Absalomu

Hapa moyo wa Absalomu unatajwa kama kifua au sehemu ya juu ya mwili.

Silaha

Hii inarejerea vyote viwili silaha za kuvaliwa kwa kujilinda na silaha za kumshambulia adui.

2 Samuel 18:16

likarudi kutoka kuwafuatia Israeli

Hapa "Israeli" inarejerea kwa jeshi la Waisraeli.

Kisha Yoabu akapiga tarumbeta na jeshi likarudi kutoka kuwafuatia Israeli, hivyo Yoabu akalirudisha jeshi

Hii inaelezea alichokiagiza Yoabu kwa kupinga tarumbeta. Yaweza pia kutafsiriwa kuwa "kisha Yoabu akapiga tarumbeta kuwarudisha wanajeshi na jeshi likarudi kutoka katika kuwafuata Israeli"

Walimchukua Absalomu na kumtupa

"Walichukua mwili wa Absalomu na kuurusha shimoni"

wakaufukia mwili wake chini ya rundo kubwa la mawe

Baada ya kuuweka mwili wake shimoni waliufunika kwa rundo la mawe.

Wakati Israeli wote

Hapa "Israeli wote" inarejerea kwa askari wa Kiisraeli. Neno "kimbia" lamaanisha kuondoka.

2 Samuel 18:18

Bonde la Mfalme

Hili ni jina la eneo.

Sina mwana wa kuchukua kumbukumbu ya jina langu

Absalomu anatumia kifungu "jina langu" kujitaja mwenyewe na familia yake.

hivyo inaitwa Mnara wa Absalomu hata leo

Hii yaweza kuelezwa kuwa hivyo watu wakaiita nguzo ya Absalomu tangu siku hiyo.

Hata leo hii

Hii inamaanisha wakati kitabu kinaandikwa.

2 Samuel 18:19

Sadoki

Hili ni jina la mwanamme.

Ahimaasi

Hili ni jina la mwanamme

niende kwa mfalme na habari njema

Hapa Ahimaasi anazungumzia kukimbia na kwenda kumwambia mfalme habari njema kama vile habari njema ilikuwa ni kitu alichokibeba.

mkono wa adui zake

Hapa "mkono" unamaanisha kutawala. Yaani "kuwatawala adui"

mchukua habari

"Anaye toa taarifa"

Hautachukua taarifa

Hii inamaanisha kutokupeleka taarifa kwa mfalme.

2 Samuel 18:21

mwambie mfalme ulichokiona

Yoabu anamwambia kwenda na kumwambia mfalme kuhusu habari ya vita.

2 Samuel 18:24

Basi

Neno hili limetumika hapa kuonesha mwisho wa habari na kuana kwa sehemu nyingine katika habari.

na kuinua macho yake

Hapa mlinzi kuona jambo inazungumzwa kana kwamba aliinua macho yake.

Anahabari kinywani

Hapa mfalme anaongelea mtu mwenye taarifa kama vile taarifa ilikuwa ni kitu kilichokaa kinywani mwake.

2 Samuel 18:26

Nadhani kukimbia kwake mtu aliye mbele ni kama kukimbia kwake Ahimaasi mwana wa Sadoki

Mlinzi analinganisha jinsi mtu anavyokimbia kama jinsi Aimaasi anavyokimbia kudhani kwamba anaweza kuwa yeye.

Ahimaasi... Sadoki

Haya ni majina ya wanaume

2 Samuel 18:28

akainama yeye mwenyewe uso wake chini mbele ya mfalme

Alifanya hivi ili kumweshimu Mfalme.

Atukuzwe Yahwe

"Atukuzwe Yahwe." Hapa "kubarika inamaanisha kutukuza.

watu walioinua mkono wao kinyume cha bwana wangu mfalme

Hapa Ahimaasi anazungumzia watu wanaompinga mfalme kama vile walikuwa wakiinua mikono yao juu yake.

fujo kubwa

Hii inamaanisha kuwa watu walikuwa wakifanya mambo kama hayakuwa sawa

Geuka kando

"Toka njiani" au "simama kando"

2 Samuel 18:31

Inuka kinyume

Inamaanisha kupinga.

Adui wa bwana wangu mfalme,... wawe kama huyo kijana

Mkushi anatumia kulinganisha kama njia laini ya kumwambia mfalme juu ya kifo cha Absalomu.

kuhuzunika

kuchanganyikiwa

2 Samuel 19

2 Samuel 19:1

Yoabu aliambiwa

Yaweza kuelezwa kuwa kuna mtu alimwambia Yoabu.

Tazama

Hii inavuta makini ya mtu kwa ajili ya kifuatacho.

Hivyo siku ile ushindi uligeuzwa kuwa maombolezo kwa jeshi lote

Hii inamaanisha kwamba jeshi lote liliomboleza badala ya kusherehekea.

2 Samuel 19:3

kama watu waonao haya baada ya kukimbia vitani

Mwandishi analinganisha jinsi askari alivyokuwa akiingia mji kama ambavyo askari wanavyokwenda baada ya kukimbia vita. Hii inamaanisha kwamba walijisikia kuaibika.

Nyemelea

Kwenda bila kutakawengine wakuone

Mfalme alifunika uso wake

Hii ni njia ya kuonesha huzuni na maombolezo.

2 Samuel 19:5

Leo umeziaibisha nyuso za askari wako

Hapa askari wanatajwa kwa nyuso zao kusisitiza jinsi ambavyo wangeficha nyuso zao kwa sababu ya aibu.

Siyo kitu kwako

Kifungu hiki kimetiwa chumvi, lakini kinaonesha uthamani mdogo alionao Daudi kwa jeshi lake.

kame Absalomu angesalia na sisi sote tungekufa hilo lingekufurahisha

mwandishi anaonesha hali ya kuhisi.

2 Samuel 19:7

Naapa kwa Yahwe

Yoabu anafanya nadhiri madhubuti.

Usipokwenda, hakuna mtu hata mmoja atakayebaki

Hii inamaanisha kwamba askari wangebaki iwapo tu Daudi angekwenda.

Hakuna atakayesalia

Hii inaonesha wao kubaki watiifu kwake.

Wote wakaambiwa

Hii inaweza kuelezwa kuwa wengi wao.

Tazama

Hii imetumika kuvuta makini ya mtu kwa ajili ya habari inayofuata.

Watu wote

Hapa "watu" inahusu waliomfuata Daudi.

Israeli walikimbia kila mtu nyumbani kwake

Hapa "Israeli" inahusu askari wa Waisraeli waliomfuata Absalomu.

2 Samuel 19:9

kutoka katika mkono wa adui zetu

Hapa "mkono" unamaanisha umiliki.

kutoka katika mkono wa Wafilisiti

Hapa "mkono" unamaanisha umiliki. Yaani kutoka chini ya miliki ya Wafilisiti.

kuikimbia nchi mbele ya Absalomu

Hii inamaanisha aliikimbia nchi mbele ya Absalomu.

Amekufa vitani

"alikufa vitani"

kwa nini hatuongei juu ya kumrudisha mfalme tena

Hii inamaanisha wanapaswa kuangalia uwezekano wa kumrudisha Daudi kwa kuwa Absalomu alikuwa amekufa.

mfalme

Inamrejerea Daudi

2 Samuel 19:11

akapeleka kwa Sadoki na Abiathari

Hii inamaanisha kwamba Daudi alipeleka mjumbe kwa Sadoki na Abiathari.

Kwa nini ninyi mmekuwa wa mwisho kumrudisha mfalme kwenye kasri lake?

Swali hili linaulizwa kuwakemea wazee wa Yuda. Yaweza kuwa "mngekuwa wa kwanza kumrudisha mfalme, siyo watu wa Israeli."

kwa vile usemi wa Israeli wote unamtaka mfalme arudi

Neno "ongea" ni nomino dhahania linaloweza kuelezwa kwa kitenzi "ongea" au "sema"

Kumrudisha mfalme katika kasiri lake

Hapa kurejesha mamlaka ya mfalme yanazungumzwa kama vile kumrudisha katika makao yake.

Ninyi ni ndugu zangu, nyama na mfupa wangu

Hapa mfalme anaeleza jinsi wanavyohusiana kwa kusema kwamba wana mwili na mfupa mmoja. Lakini pia maneno "ninyi ni" yaweza kuongezwa katika kirai cha pili.

Kwa nini basi mmekuwa wa mwisho kumrudisha mfalme?

Hili ni swali la pili na pia ni karipia kwa wazee wa Yuda.

2 Samuel 19:13

Amasa

Hili ni jina la mwanamme

Je wewe si mwili na mfupa wangu?

Daudi anatumia swali kusisitiza uhusiano wao.

mwili wangu na mfupa wangu

Hapa Daudi anawazungumzia kuhusiana kwao kwa kusema kwamba wana mwili na mfupa mmoja.

Mungu anifanyie hivyo

Huu ni usema unaomaanisha Mungu kumwua

Akaishawishi mioyo

Hapa utiifu wa watu unazungumzwa kama "mioyo".

Kama mtu mmoja

Hii inazungumzia watu kuungana katika utiifu wao kwa mfalme kama vile walikuwa walikuwa na nia moja.

walipeleka kwa mfalme

Hii inamaanisha kwamba walipeleka ujumbe kwa mfalme.

2 Samuel 19:16

Gera... Siba

Haya ni majina ya wanaume.

Bahurimu

Hili ni jina la sehemu

watu elfu moja... wana kumi na watano... watumishi ishirini

"watu 1,000... wana 15... watumishi 20"

mbele ya mfalme

Hii inamaanisha kwamba mfalme alikuwepo na alikuwa anafahamu kilichokuwa kinaendelea.

2 Samuel 19:19

Kukumbuka

Ni kukumbuka jambo

mtumishi wako

Hapa Shimei anajitaja kwa njia hii kuonesha heshima kwa mfalme.

2 Samuel 19:21

Abishai

Hili ni jina la mwanamme

Seruya

Hili ni jina la mwanamme.

Je Shimei asife kwa hili kwa vile alivyomlaani mtiwa mafuta wa Yahweh?

Seruya alimkasirikia Shimei kwa kumlaani Daudi na anasema anapaswa kufa.

Mtiwa mafuta wa Yahwe

Hii inamrejerea Daudi. Inamaana kwamba Daudi alikuwa mfalme aliyetiwa mafuta na Yahwe

Nifanye nini nanyi... hata leo mkawa adui zangu?

Daudi anatumia swali hili kumkemea Abishai. Hii inamaanisha kwamba hawakuwa na sababu ya kuwa adui.

Je mtu yeyote atauawa leo katika Israeli? Kwani sijui kama leo mimi ni mfalme juu ya Israeli?

Daudi anatumia swali kuendelea kumkemea Abishai. Kumaanisha "Hakuna mtu atakayeuawa leo katika taifa la Israeli.

Je kuna mtu atakayeuawa

Kifungu "kuuawa" inamaanisha kunyongwa au kuuawa.

Kwani sijui kama leo mimi ni mfalme juu ya Israeli?

Maana yake yaweza kuwa 1) "Ninajua kwamba mimi bado ni mfalme wa Israeli." 2) "Leo mimi ni mfalme juu ya Israeli!"

2 Samuel 19:24

Mefiboshethi

Hili ni jina la mwanaume

Hakuwa ameivalisha miguu yake

"Hakuwa ameitunza miguu yake." Miguu ya Mefiboshethi ilikuwa na ulemavu. Kifungu kinaonesha hakuwa ameitunza miguu yake vizuri.

Kwa nini haukwenda nami, Mefiboshethi?

Daudi anazungumzia kwa nini hakwenda naye pale yeye na watu waliomfuata walipoondoka Yerusalme.

2 Samuel 19:26

Siba

Hili ni jina la mwanamme

Bwana wangu mfalme ni kama malaika wa Mungu

Hapa hekima ya Daudi inalinganishwa na hekima ya malaika.

Fanya lililojema machoni pako

Hii inamaanisha kufanya unalodhani kuwa sawa.

Kwa maana nyumba yote ya baba yangu walikuwa maiti mbele ya bwana wangu mfalme

Mefiboshethi anazungumza jinsi ndugu zake walivyostahili kuuawa kama vile tiyari walikuwa wameuawa na walikuwa wafu.

nyumba ya bwana wangu

Hii inawahusu ndugu wa baba yake.

hiyo nililiye haki gani zaidi kwa mfalme?

Mefiboshethi anatumia swali kusisitiza kwamba hana haki ya kuomba chochote kwa mfalme.

2 Samuel 19:29

Kwa nini kueleza yote zaidi?

Daudi anatumia swali kumwambia haitajiki kuendelea kuongelea mgogoro wake na Siba.

2 Samuel 19:31

Berzilai

Hili ni jina la mwanaume

Rogelimu... Mahanaimu

Haya ni majina ya maeneo

Mgileadi

Hili ni jina la ukoo katika Israeli.

Yordani

Mto Yordani

Miaka themanini

"Umri wa miaka 80"

Kuhudumia

"kuandaa"

2 Samuel 19:34

Kwani kuna siku ngapi zilizosalia maishani mwangu, hata niende na mfalme huko Yerusalemu?

Hapa Berzillai anamaanisha kwamba yeye ni mzee na kwamba hakuna haja ya yeye kumsindikiza Daudi. Yaweza kumaanisha kuwa sitaweza kuishi muda mrefu. Kwa hiyo hakuna haja ya kwenda na mfalme huko Yerusalem.

Miaka themanini

"umri wa miaka 80"

Kwa nini basi mtumishi wako awe mzigo kwa bwana wangu mfalme?

Hapa Berzilai anamaanisha kwamba hapendi kuwa mzigo kwa mfalme.

Je naweza kutofautisha kati ya mema na mabaya?

Berzilai anatumia maswali kusisitiza kwa nini hapendi kwenda Yerusalemu. "Mema" na "mabaya" yanamaanisha kinachotamaniwa na kisichotamaniwa.

Je mtumishi wako aweza kuonja anachokula na kunywa?

Barizilai anatumia maswali ya kusisitiza kwa nini haitaji kwenda Yerusalemu.

Je naweza kuisia zaidi sauti za wanaume na wanawake waimbao?

Berizilai anatumia maswali ya msisitizo kwa nini hapendi kwenda Yerusalemu.

Kwa nini basi mtumishi wako awe mzigo kwa bwana wangu mfalme?

Berizilai anatumia swali kusisitiza kwamba hafikirii kwama anapaswa kwenda na mfalme huko Yerusalemu.

Kwa nini mfalme anilipe kwa thawabu hiyo?

Berizilai anatumia swali kusisitiza kwamba hajui ni lini mfalme angemlipa kwa njia hii.

2 Samuel 19:37

Maelezo ya Jumla

Berzilai anaomba kwamba Kimhamu aachwe kuchukua nafasi yake.

Kimhamu

Hili ni jina la mwanaume

katika kaburi la baba na mama yangu

Hii haimaanishi kwamba anataka kufa mara tu baada ya makaburi yao, lakini anamaanisha kwamba anataka afe katika mji walipozikwa.

Yeye avuke

Hii inamaanisha kuvuka Mto Yordani.

2 Samuel 19:38

Kimhamu atavuka nami.

Hii inarejerea kuvuka Mto Yordani.

2 Samuel 19:40

akavuka kuelekea Gilgali

Walivuka Mto Yordani kuelekea Gilgali.

Kimhamu

Hili ni jina la mwanamme

kumleta mfalme

"kumsindikiza mfalme." Walivuka Mto Yordani.

Jeshi la Yuda lote na nusu ya jeshi la Israeli likamleta mfalme.

"Jeshi la Yuda lote na nusu jeshi ya Israeli likamleta mfalme"

Kwa nini ndugu zetu, watu wa Yuda... na watu wote wa Daudi pamoja naye?

Watu wa Israeli wanatumia swali hili kuonesha kwama wajisikia kwamba wamesalitiwa na ndugu zao wa Yuda.

Kukutolosha

Waisraeli wanazungumza jinsi watu wa Yuda walivyomsindikiza mfalme kuvuka mto kama vile mfalme alikuwa kitu kilichoibwa kisicho chao.

Yordani

Mto Yordani

2 Samuel 19:42

Kwa nini basi mkasirike juu ya hili?

Watu wa Israeli wanauliza swali hili kuwakemea watu wa Israeli.

Je sisi tumekula chochote ambacho mfalme amekitoa? Je ametupa zawadi yoyote?

Watu wa Yuda kama swali linavyoonesha wanaonesha kwamba hawajachukua chochote kwa mfalme.

Hata hivyo tuna haki zaidi kwa mfalme kuliko ninyi

"Tuna madai makubwa kwa Daudi kuliko ninyi." Yaani "tuna haki zaidi ya kumhudumia mfalme na kuwa naye kuliko ninyi"

Kwa nini basi kutudharau?

Waisraeli wanauliza swali hili kuonesha hasira yao. Yaweza kuwa "hamkupaswa kutudharau hivyo!"

Je hatukuwa wa kwanza kupendekeza kumrudisha mfalme wetu?

Watu wa Israeli wanauliza swali hili kuwakumbusha na kuwakemea watu wa Yuda.

Lakini maneno ya watu wa Yuda hata yakawa makali kuliko maneno ya watu wa Israeli.

Hapa "maneno" yarejerea mazungumzo ya watu wa Yuda.

2 Samuel 20

2 Samuel 20:1

kuwa mahali pamoja

Hii inarejerea mji wa Gilgali.

Sheba... Bikri

Haya ni majina ya wanaume.

Sisi hatuna sehemu katika Daudi, wala hatuna urithi katika mwana wa Yese

Maelezo haya yote yanamaanisha kitu kimoja. Shiba anasisitiza kwamba yeye na makabila ya Israeli hawana uhusiano na Daudi. Yaani urithi wa Daudi na familia ya baba yake hawana uhusiano na Israeli.

2 Samuel 20:3

kulitunza kasiri

Hapa kifungu "kutunza" inamaanisha kuangalia.

nyumbani chini ya ulinzi

Ikiwa nyumba iko "chini ya ulinzi" inamaanisha kuna mlinzi aliyepo katika nyumba.

walikuwa imefungwa

Inamaana hawakuruhusiwa kutoka ndani

wajane

Hawa ni wanawake ambao waume zao wamefariki.

2 Samuel 20:4

Amasa

Huyu ni jemedari wa jeshi la Daudi.

2 Samuel 20:6

Abishai

Huyu ni jemedari mwingine wa jeshi la Daudi.

Hasitudhuru zaidi

"hasituumize zaidi"

watumishi wa bwana wako, askari wangu

Kifungu "askari wangu" inafafanua "watumishi" wapi. Daudi anajitaja mwenyewe kama "bwana wako" kama njia rasmi ya kuongeza na mtu mwenye cheo cha chini.

kumfuatia

"kufukuza mtu"

mbali na upeo wa macho yetu

Hapa Daudi anataja jeshi lake kwa uoni wao kusisitiza kwamba Shiba na watu wake wangejificha hata wasiwakamate.

ataona miji yenye ngome

Hii inamaana kwamba Shiba na watu wake wangeingia katika miji hii na kujificha kutoka jeshi la Daudi. Neno "yeye" linasimama badala ya Shiba lakini linawarejerea wote Shiba na watu wake.

Wakelethi... Wapelethi

Haya ni majina ya makundi ya watu waliokuwa wakimlinda Mfalme Daudi.

2 Samuel 20:8

Walipokuwa

"Walipokuwa Yoabu na watu wa Yuda"

mkanda

mshipi wa ngozi au kitu kingine kilichotengenezwa kufunga vazi au silaha.

upanga ukadondoka

upanga ukaanguka

upanga ukadondoka

Yoabu aliuacha upanga uanguka ili kumpumbaza Amasa kwa kufikiri kwamba Yoabu hakuwa na silaha, hata amruhusu Yoabu kumkaribia.

2 Samuel 20:9

binamu yangu

Amasa alikuwa mwana wa dada wa mama wa Yoabu.

kwa utaratibu

"kwa upole"

akakishika kidevu cha Amasa kwa mkono wake wa kulia ili ambusu

Hii ilikuwa njia ya kawaida a watu kusalimiana.

jambia

upanga mfupi ambao ni rahisi kuuficha ulikuwa mapigano ya karibu na mauaji.

matumbo kumwagika

utumbo ulitoka nje.

2 Samuel 20:11

aliye kwa ajili ya Daudi

Kuwa "kwa ajili" ya mtu inamaanisha kumuunga mkono.

Amasa akalala akigaagaa katika damu yake

Amasa alikuwa akaijivingirisha katika damu yake, lakini kwa wakati huu yawezekana alikwisha kufa. Inaelezwa hivi kuonesha mwili wake ulivyoonekana.

watu wote wakasimama... kumkaribia wakasimama

Inaanisha waliacha kutembea na kushangaa maiti ya Amasa.

Alimbeba Amasa

"aliubeba mwili wa Amasa"

Baada ya Amasa kuondolewa njiani

Hii yaweza kuelezawa kuwa baada ya mtu kuuondoa mwili wa Amasa njiani.

katika kumfuatia

Nomino dhahania yaweza kuelezwa kama kitenzi.

2 Samuel 20:14

Sheba akapita

Hapa "Sheba" inarejerea kwa wote Sheba na jeshi lake.

Abeli wa Bethi Maaka

"Abeli wa Bethi Maaka." Majina yote yanahusu sehemu moja na yaweza kuunganishwa. Ni mji karibu na kabila ya Yuda.

Wa Waberite

Hili ni jina la kundi la watu.

na pia kumfuata Sheba

"Walimfuata Sheba pia"

kujenga buruji

Hii inamaanisha walitumia silaha ya kubomolea kuungonga ukuta. Chombo hiki kilikuwa ni mti mrefu wenye ncha or kuwekewa ncha ya chuma. Kilishikiliwa na watu kadhaa ambao gonga ncha kwenye ukuta.

Walimpata

"Yoabu na askari walimpata"

dhidi ya ukuta kinyume cha mji

"dhidi ya ukuta wa mji"

Sikilizeni, sikilizeni tafadhari

Kurudia kwa neno "sikilizeni" kunasisitiza ombi la mwanamke.

2 Samuel 20:17

Sikiliza maneno ya mtumishi wako

Mwanamke anajitaja kama "mtumishi wako." Hii in njia laini ya mtu kuongea na mtu mwenye mamlaka.

na ushauri huo ungemaliza jambo

"na ushauri huo ungetatua tatizo"

wenye amani na uaminifu zaidi katika Israeli

Maneno yanayokosekana waweza kuongeza kuwa wa amani na mji mwaminifu zaidi katika Israeli"

Mji mama katika Israeli

Hii inamaanisha umuhimu wa mji katika nchi ya Israeli kama vile ulikuwa mji wenye heshima kama mama mwenye heshima.

Kwa nini unataka kuumeza urithi wa Yahwe?

Hapa mwanamke anatumia swali kupendekeza kwa Yoabu cha kuacha kufanya.

Kuumeza

Mwanamke anazungumzia adui kuuaribu mji kama ulikuwa chakula cha kumezwa.

urithi wa Yahwe

Mji unaoneshwa kama urithi wa Yahwe kusisitiza kwamba unamilikiwa na Yahwe.

2 Samuel 20:20

Iwe mbali, iwe mbali nami, hata

Hapa anarudia kifungu hiki kusisitiza kwamba asingefanya vile.

hata nikameze au kuharibu

Hii inamaanisha kuharibu mji.

kumeza au kuharibu

Katika vifungu vyote maana yake ni kuharibu. Katika kifungu cha kwanza "kuharibu" inasemwa kama ndiko "kumeza." Hii yaweza kuunganishwa.

ameinua mkono wake dhidi ya

Hii inamaanisha kuasi na kupigana na mtu fulani.

Mtoeni peke yake

Yoabu anawambia watu wa mji kumtoa Sheba peke yake.

Nitauacha mji

Hapa "mimi" inawataja wote Yoabu na askari.

Kichwa chake kitarushwa

Yaweza kuwa tutakurushia kichwa chake.

Kisha mwanamke akawaendea watu wa mji katika hekima yake

Inamaanisha mwanamke alitenda kwa busara na kuongea na watu wake walichopaswa kufanya.

kila mtu nyumbani kwake

"Kila mtu alirudi nyumbani kwake"

2 Samuel 20:23

Basi

Inaonesha mkato katika habari. Sehemu inayofuata inatoa mazingira ya watu waliomtumikia Mfalme Daudi

Yoabu alikuwa juu... Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa juu... Adoramu alikuwa juu

Kifungu "alikuwa juu" kinaonesha kuwa na mamlaka juu ya kundi la watu.

Yehoyada... Yehoshafati... Ahiludi

Haya ni majina ya wanamme.

Wakerethi... Wapelethi

Hawa walikuwa walinzi binafsi wa Daudi

Watu waliofanya kazi ya shuruti

"watumwa"

Adoramu... Sheva... Ira

Haya ni majina ya wanaume

Muyairi

Hili ni jina la kundi la watu.

2 Samuel 21

2 Samuel 21:1

alitafuta uso wa Yahwe

"Uso" inamaanisha uwepo wa Yahwe. Inamana Daudi aliomba kwa Yahwe kwa ajili ya njaa.

kwa sababu ya Sauli na familia yake ya mauaji

Sauli alikuwa ameuwauwa Wagibioni wengi, na wazao wake wana hatia kwa sababu ya dhambi hii.

2 Samuel 21:2

Basi

Inaonesha kuisha kwa habari na kutoa mazingira ya habari inayofuata kuhusu Wagibeoni.

Niwatendee nini? Nifanyeje upatanisho... ahadi?

Mistari hii miwili ina maana inayofanana. Yaani "Nifanyeje kuondoa dhambi hii, ili mwabariki watu wa Yahwe, waumilikio wema wake na ahadi zake?

2 Samuel 21:4

Si jambo la fedha wala dhahabu

"Pesa hazitaweza kutatua tatizo"

2 Samuel 21:5

aliyepanga kinyume chetu

"aliyefanya mipango dhidi yetu"

haya na tupewe watu saba kutoka katika uzao wake

Yamaanisha "waruhusu watu wako kutopa wazao wake saba"

Tutawatundika

"tutawanyonga kwa kuwatundika"

Katika Gibea ya Sauli

Sauli alikuwa anatoka katika mji wa Gibea.

Aliyeteuliwa na Yahwe

Yaweza kuwa "atakayechaguliwa na Yahwe"

2 Samuel 21:7

Mefiboshethi

Alikuwa mwana wa Yonathani.

Rispa... Aiya

Rispa alikuwa mwanamke na babaye aliitwa Aiya.

Amoni na Mefiboshethi... Adrieli... Barzilai

Haya ni majina ya wanaume. Huyu siyo Mefiboshethi mwana wa Yonathani.

Mikali

Hili ni jina la binti wa mfalme Sauli na alikuwa mke wa kwanza wa Daudi.

Mmeolathi

Hili ni jina la kundi la watu.

Akawakabidhi katika mikono ya Wagibeoni.

"mikono ya wagibeoni" inamaanisha Wagibeoni.

Wakauawa

Wagibeoni waliwauwa.

2 Samuel 21:10

Rispa... Aiya

Rispa alikuwa mwanamke na babaye aliitwa Aiya

Daudi aliambiwa

Mtu fulani alimwambia Daudi

2 Samuel 21:12

Yabeshi Gileadi

Huu ulikuwa ni mji katika eneo la Gibea.

Eneo la wazi

Hili ni eneo karibu na lango la mji ambapo watu walifanya kazi mbalimbali.

Bethi Shani

Hili ni jina la eneo

Gilboa

Hili ni jina la mlima

Waliokuwa wametundikwa

"Ambao Wagibeoni waliwanyonga kwa kuwatundika"

2 Samuel 21:14

Zela

Hili ni jina la mji huko Benjamini

Kishi

Hili ni jina la mwanamme.

Babaye

"baba yake Sauli"

2 Samuel 21:15

Ishibibenobu

Hili ni jina la mwanamme.

shekeli mia tatu

"shekeli 300"

Abishai mwana wa Seruya

Abishai na Seruya ni majina ya wanaume

usije ukaizima taa ya Israel

"Taa ya Israeli" ni usemi unaomaanisha uongozi wa Daudi na kama angekufa watu wangekosa mwelekeo sahihi.

2 Samuel 21:18

Ikawa baada ya haya

Kifungu kinaonesha mwanzo wa sehemu inayofuata

Gobu

Hili ni jina la mji.

Sibekai... Safu... Elhanani mwana wa Jari... Goliathi

Haya ni majina ya wanaume.

Muhushathi... Mrefai... Mbethlehemu... Mgiti

Haya ni majina ya wakundi ya watu.

Mrefai

Kundi hili la watu walijulikana kwa ushujaa wao mkubwa.

ambaye mkuki wake ulikuwa kama mti wa mfumaji

Mtu alipokuwa anafuma nguo alipitisha nyuzi katika ndoano zilizounganishwa katika mti ulioitwa "mti wa mfumaji." Hii inamaana kwamba mkuki wa Goliathi ulikuwa siyo mkuki wa kawaida.

2 Samuel 21:20

Numba ishirini na nne

Numba ina - "vidole 24 vya mikono na miguu kwa pamoja"

Mrefai

Kundi hili la watu walijulikana kwa ushujaa wao mkubwa.

Yonathani mwana wa Shama

Huyu alikuwa nduguye Daudi.

waliuawa kwa mkono wa Daudi na kwa mkono wa askari wake

"kwa mkono wa" humaanisha "kupitia" au "kwa". Maana yake ni Daudi na watu wake waliwaua.

2 Samuel 22

2 Samuel 22:1

Maelizo ya Jumla:

Wimbo wa Daudi kwa Yahwe unaanza. Anatumia usambaba kusisitiza akisemacho

katika mkono wa adui zake wote na katika mkono wa Sauli

Huu ni mwendelezo kutoka maadui na kwenda kwa adui maalumu wa Daudi, Mfalme Sauli.

kutoka mkono wa

"Inamaanisha kutoka katika nguvu ya"

Yahwe ni mwamba wangu, ngome yangu

Usemi huu unamaanisha mwendelezo katika sehemu, "mwamba" kwa ujumla "ngome." Ngome inajengwa kwa mawe mengi makubwa. Hii inamaanisha kwamba Yahwe ananguvu za kulinda watu wake katika madhara.

2 Samuel 22:3

Maelezo ya Jumla:

Wimbo wa Daudi kwa Yahwe unaanza. Anatumia usambaba kusisitiza akisemacho

Mungu ni mwamba wangu... Yeye ni ngao yangu, pembe ya wokovu wangu, ngome yangu.

Semi hizi zote ni alama za nguvu na uwezo wa Mungu. Zinasisitiza uwezo wa Mungu wa kulinda na kuokoa watu wake

Astahiliye kusifiwa

Yaani "anayestahili kupokea sifa"

Nitaokolewa na adui zangu

"Ataniokoa na adui zangu"

2 Samuel 22:5

Maelezo ya Jumla:

Wimbo wa Daudi kwa Yahwe unaanza. Anatumia usambaba kusisitiza akisemacho.

Maana mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maji ya uharibifu yakanishinda

Daudi anawalinganisha waovu waliotaka kumwua kama mafuriko ya maji yatakayo kumzamisha. Mistari hii miwili ina maana moja na imetumika kwa msisitizo.

Maana mawimbi ya mauti yalinizunguka

Hii ni picha ya maji yaendayo kasi na kuharibu kila kitu yapitapo.

Vifungo vya kuzimu vilinizunguka; kamba za mauti zikaninasa

Daudi anazungumzia mauti na kuzimu kama watu watakao kumnasa kama mwindaji anasavyo mnyama. Vifung viwili hivi vina maana moja na imetumika kwa msisitizo.

2 Samuel 22:7

Maelezo ya Jumla:

Wimbo wa Daudi kwa Yahwe unaendelea. Anatumia usambaba kusisitiza akisemacho

Katika shida yangu

"katika taabu zangu kubwa"

akaisikia sauti yangu katika hekalu lake,

Daudi anamaanisha hekalu la mbinguni anapoishi Yahwe. Hekalu la duniani lilikuwa bado kujengwa.

kilio changu cha msaada kikafika masikioni mwake

Usemi wa "masikio yake" inaonesha Yahwe akisikiliza kilio cha Daudi kwa msaada.

2 Samuel 22:8

Maelezo ya Jumla:

Wimbo wa Daudi kwa Yahwe unaendelea. Anatumia usambaba kusisitiza akisemacho

Kisha nchi ilitikisika... ikawashwa kwayo

Hili ni jibu la Yahwe kwa kilio cha Daudi msaada kutoka kwa adui zake. Daudi anatumia taswira ya dunia kutikisika na moto kutoka kwa Yahwe kusisitiza hasira kari ya Yahwe.

Dunia ilitikisika... mbingu zikatetemeka

Daudi anazungumzia mitizamo hii miwili kuhusisha kila kitu katika uumbaji.

na ilitikiswa , kwa sababu Mungu alikuwa na hasira.

Hii yaweza kumaanisha "kwa sababu hasira ya Mungu ilizitikisa."

mianzi ya pua yake... kinywa chake

Daudi anamzungumzia Yahwe kama vile alikuwa na sehemu hizi za wanadamu.

Makaa yaliwasha kwayo

Hapa hasira ya Yahwe inalinganishwa na moto, uliosababisha makaa kuwashwa.

2 Samuel 22:10

Maelezo ya Jumla:

Wimbo wa Daudi kwa Yahwe unaendelea. Anatumia usambaba kusisitiza akisemacho

Alizifungua mbingu... akamwaga mawingu angani

Daudi anazungumzia njia za Yahwe kwa kumwokoa Daudi kutoka kwa adui zake kama mawingu ya dhoruba yakusanyikayo juu ya sehemu. Hii inasisitiza nguvu za Mungu na hasira yake.

chini ya miguu yake

Daudi anamzungumzia Mungu kama ana miguu ya watu.

Alionekana katika mawingu ya upepo

Yaweza kuwa "alionekana juu ya mawingu ya upepo"

mawingu ya upepo

Hii inaonesha upepo kama ulikuwa ni ndege

Na akafanya giza hema kumzunguka

Giza alilolifanya Yahwe linalinganishwa na hema limfichalo kabisa.

2 Samuel 22:13

Maelezo ya Jumla:

Wimbo wa Daudi kwa Yahwe unaendelea. Anatumia usambaba kusisitiza akisemacho

Kutoka katika radi mbele zake... miale ya radi na kuwasambaratisha

Daudi anaendelea kumweleza Yahwe, anayemlinganisha na kimbunga, akija kumwokoa kutoka kwa adui. Hii inasisitiza nguvu ya Mungu na hasira yake kwa adui wa Daudi.

Makaa ya moto yalidondoka mbele zake kutoka katika radi

Maana yake yaweza kuwa 1) "kutoka katika mwanga mwangavu alituma makaa yawakayo" au 2) "kutoka katika mwangaza wake alituma radi"

Aliyejuu sana alipiga kelele. Akapiga mishale.

Daudi anamweleza Yahwe akifanya matendo anayoweza kufanya mtu.

Alipiga mishale... miale ya radi

Daudi analinganisha radi kutoka kwa tufani ya Yahwe na mishale wangetumia askari.

2 Samuel 22:16

Maelezo ya Jumla:

Wimbo wa Daudi kwa Yahwe unaendelea. Anatumia usambaba kusisitiza akisemacho

Ndipo njia za maji zilipoonekana... pumzi ya pua zake

Yahwe alipopiga kelele katika shambulio lake kwa adui za Daudi, inalinganishwa na nguvu zake za kufanya mambo katika vilindi vya bahari na nchi. Hii inaonesha uwezo wake mkuu na hasira yake kali.

misingi... ilifunuliwa

Daudi analinganisha hasira ya Yahwe na miondoka ya ardhi.

2 Samuel 22:17

Maelezo ya Jumla:

Wimbo wa Daudi kwa Yahwe unaendelea. Anatumia usambaba kusisitiza akisemacho

kutoka katika vilindi vya maji

Daudi analinganisha adui zake na mafuriko yanayotishia kumzamisha.

Aliokoa kuatoka kwa adui yangu mwenye nguvu.

Adui wa Daudi walikuwa na nguvu. Alimsifu Mungu kwa kumkomboa kutoka kwa adui zake wote.

2 Samuel 22:19

Maelezo ya Jumla:

Wimbo wa Daudi kwa Yahwe unaendelea. Anatumia usambaba kusisitiza akisemacho

Walikuja kinyume changu siku ya shida yangu

"Adui zangu walipigana nami nilipokuwa katika shida kubwa"

siku ya shida yangu

Neno "siku" linawakilisha muda Daudi alipokuwa katika shida.

Lakini Yahwe alikuwa msaada wangu

"lakini Yahwe alinisaidia"

mahali palipo na nafasi

Hapa ni mahali pasipo na hatari na adui wasingemnasa.

kipimo cha usafi wa mikono yangu

Hapa "usafi wa mikono yangu" inamaanisha kitu kimoja "haki"

2 Samuel 22:22

Maelezo ya Jumla:

Wimbo wa Daudi kwa Yahwe unaendelea

Nimezitii njia za Yahwe

"Njia za Yahwe" inamaanisha jinsi Yahwe anavyotaka watu wake kuenenda. Hii inamaanisha Daudi alifanya kile Yahwe alichotaka afanye.

mekuwa mbele yangu

Hii inamaanisha Daudi mara kwa mara husoma na kutafakari maagizo ya Mungu

2 Samuel 22:24

Maelezo ya Jumla:

Wimbo wa Daudi kwa Yahwe unaendelea

Nimejiepusha na dhambi

Hii ni kuchagua kutomtenda dhambi Yahwe

kwa kadiri ya usafi wangu mbele zake

"Usafi wangu" inamaanisha kilekile "utakatifu wangu"

2 Samuel 22:26

Maelezo ya Jumla:

Wimbo wa Daudi kwa Yahwe unaendelea

lakini kwa wakaidi unajionesha kuwa mkaidi

"kaidi" inamaanisha kuwa mkaidi, na "mpotevu" inamaanisha kutoka katika mema na haki. Inamaanisha Mungu huwashughulikia watu kwa hekima.

2 Samuel 22:28

Maelezo ya Jumla:

Wimbo wa Daudi kwa Yahwe unaendelea

macho yako ni kinyume cha wenye kiburi

"macho yako" inamaanisha anachoona Yahwe. Inamaanisha Mungu humwona mwenye kiburi.

Unawashusha chini

"unaharibu kiburi chao"

wewe ni taa yangu, Yahwe. Yahwe humlika katika giza langu.

Usemi huu unamlinganisha Yahwe na taa, inamaana Humpa Daudi nuru na msaada wa kuona mambo yanapoaribika.

2 Samuel 22:30

Maelezo ya Jumla:

Wimbo wa Daudi kwa Yahwe unaendelea

Naweza kupita vipingamizi

"Vipingamizi" vyamaanisha kundi la askari au ukuta wa mawe. Yote yamaanisha Mungu humwezesha Daudi kuwashinda adui zake.

Naweza kuruka ukuta

Daudi ametia chumvi ili kusisitiza msaada wa Yahwe.

Neno la Yahwe ni safi

"Kila anachosema Yahwe ni kweli"

Yeye ni ngao

"Ngao" yasisitiza uwezo wa Mungu kuwalinda watu wake.

2 Samuel 22:32

Maelezo ya Jumla:

Wimbo wa Daudi kwa Yahwe unaendelea.

Maana ni nani aliye Mungu isipokuwa Yahwe? Na ni nani aliyemwamba isipokuwa Mungu?

Daudi anatumia maswali kusisitiza kwamba hakuna Mungu zaidi ya Yahwe.

aliyemwamba

Daudi anamlinganisha Yahwe na mwamba kusisitiza nguvu zake na uwezo wa kuwalinda watu wake.

humwongoza asiye na hatia katika njia yake

Yahwe humlinda asiye na hatia katika usalama na kuondoa kila kinachoweza kumdhuru.

2 Samuel 22:34

Maelezo ya Jumla:

Wimbo wa Daudi kwa Yahwe unaendelea.

Huifanya myepesi miguu yangu kama kurungu na kuniweka katika vilima virefu.

Miguu ya Daudi inafananishwa na ya kurungu kwa kutiwa chumvi. Yahwe anampa Daudi nguvu za kuondoka kwa kasi na kumwandalia mahali salama kwa ulinzi na pumziko.

Mikono yangu... na vitanga vyangu

Vyote vinamrejerea Daudi.

Kupinda upinde wa shaba

Ni mtu mwenye nguvu pekee awezaye kutumia upinde ulitengenezwa kwa madini.

2 Samuel 22:36

Maelezo ya Jumla:

Wimbo wa Daudi kwa Yahwe unaendelea

hii ngao ya wokovu wako

Daudi anailinganisha nguvu ya Yahwe ya kuokoa sawa na ngao inayomkinga askari na adui yake.

Matakwa yako

Mungu alijibu maombi ya Daudi na kumpa baraka na mafanikio juu ya adui zake

7Umeitengenezea miguu yangu nafasi chini yangu

Yahwe amemweka Daudi mahala salama ambapo adui zake hawawezi kumnasa. "Miguu" inamaanisha uwezo wa Daudi wa kusimama salama.

2 Samuel 22:38

Maelezo ya Jumla:

Wimbo wa Daudi kwa Yahwe unaendelea

fuatia adui zangu

"kufukuza adui zangu"

Niliwararua na kuwasambaratisha

Daudi anajilinganisha na hayawani wakali.

chini ya miguu yangu

"Miguu" hapa inamaanisha nguvu na kumiliki ushindi juu ya adui zake.

2 Samuel 22:40

Maelezo ya Jumla:

Wimbo wa Daudi kwa Yahwe unaendelea

Unanivika nguvu kama mkanda kwa vita

Hapa nguvu atoazo Yahwe zafananishwa na mkanda unaomwezesha Daudi kufanya mambo yenye nguvu.

unawaweka chini yangu wanaoinuka kinyume changu

"ulinisaidia kuwashinda walioshindana nami"

migongo ya shingo za adui zangu

Maana yake yaweza kuwa 1) Daudi kuona migogo ya adui zake walipokimbia au 2) Daudi kuwaka mguu wake nyuma ya shingo ya adui zake baada ya kuwashinda.

niliwaangamiza kabisa

"Niliwaangazi kabisa"

2 Samuel 22:42

Maelezo ya Jumla:

Wimbo wa Daudi kwa Yahwe unaendelea

Walilia

"adui zangu walilia"

walimlilia Yahwe, lakini hakuwajibu

Muda wa hukumu ya Yahwe juu yao ilikuwa juu yao.

kama vumbi juu ya ardhi... kama matope mitaani

Inamaanisha Daudi aliwaangamiza adui zake kabisa. Vifungu hivi viwili "kama vumbi juu ya ardhi" na "kama tope mitaani" vina maana moja na vimetumika kwa msisitizo.

2 Samuel 22:44

Maelezo ya Jumla:

Wimbo wa Daudi kwa Yahwe unaendelea

kutoka katika mashutumu ya watu wangu

Hii inarejerea miongoni mwa Waisraeli walioasi dhidi ya Mfalme Daudi.

Umeniweka kama kichwa cha mataifa.

"Uliniweka kama mtawala juu ya mataifa." Hapa "mataifa" yamaanisha nchi nyingine tofauti na Israeli.

Watu ambao sikuwajua

"Wageni"

kutoka katika mashutumu ya watu wangu

Yaweza kuwa "wageni walinipigia magoti"

2 Samuel 22:47

Mwamba wangu atukuzwe. Mungu na ainuliwe

Mistari hii ina maana inayofanana na imetumika kwa msisitizo.

mwamba wangu... mwamba

Daudi anamlinganisha Yahwe na mwamba kusisitiza uwezo wake wa kuwalinda watu wake.

awawekaye watu chini yangu.

Yeye awawekaye watu chini ya utawala wangu.

Uniweka huru mbali na adui zangu

"Uliniokoa na adui zangu na kunipa heshima"

kutoka kwa watu wenye ghasia

"kutoka kwao watakao kunidhuru"

2 Samuel 22:50

Maelezo ya Ujumla

Daudi anahitimisha wimbo wake kwa Yahwe

kwa jina lako

Hapa neno "jina" inaonesha heshima ya Yahwe.

na uonesha uaminifu wake wa kiagano kwa mtiwa mafuta wake

Daudi anaweza kuwa anarejerea ahadi alizosifanya Yahwe katika 7:8

2 Samuel 23

2 Samuel 23:1

Basi

Hii inaonesha mwanzo wa sehemu nyingine ya kitabu

haya ni maneno ya mwisho

Hii inaonesha atakachokisema Daudi katika 23:1.

mtu aliyeheshimiwa sana, aliyetiwa mafuta na Mungu wa Yakobo

Hii yaweza kumaanisha: "Mtu ambaye Mungu wa Yakobo alimweshimu na kumtia mafuta"

aliyetiwa mafuta na Mungu wa Yakobo

Kutiwa mafuta kulifanywa kwa kumimina mafuta juu ya kichwa cha mtu katia kuchagua ambaye angemtumikia Mungu kama mfalme au kuhani.

Mzaburi

Huyu ni mtu aandikaye zaburi au nyimbo.

kwangu

kwa Daudi

na neno lake lilikuwa katika ulimi wangu

"juu ya ulimi wangu" ni usemi unaomaanisha Daudi.

2 Samuel 23:3

Maelezo ya Ujumla

Hii inaendeleza maneno ya mwisho ya Daudi.

Mungu wa Israeli alinena, Mwamba wa Israeli... nami

Hapa "Mungu wa Israeli" na "Mwamba wa Israeli" ni yuleyule. Vingungu vyote viwili vinazungumzia jambo moja la msingi. Daudi anamlinganisha Mungu na mwamba kusisitiza uwezo wake wa kulinda watu.

Atawalaye kwa haki juu yangu, atawalaye katika hofu ya Mungu

Mistari miwili hii inasema kwamba mfalme atamweshimu Mungu na kufanya Mungu anachotaka.

kwa hofu ya Mungu

"kumweshimu Mungu"

Atakuwa kama mwanga wa asubuhi...nuru ya jua baada ya mvua

Hapa Mungu anamlinganisha mfalme na nuru ya asubuhi na nuru ya jua baada ya mvua. Zote ni njia za kusema mfalme huyu angekuwa wa kupendwa na Mungu na baraka kwa watu. Vifungu hivi viwili vina maana inayofanana na vimetumika kwa msisitizo.

2 Samuel 23:5

Maelezo ya Ujumla

Hii inaendeleza maneno ya mwisho ya Daudi

Hakika, je familia yangu haiko hivi mbele za Mungu?

Hapa Daudi anakubaliana ya Mungu.

Je yeye hajafanya... njia?

Daudi anakubari kwamba Mungu amefanya agano naye.

taratibu na hakika

Hii inamaanisha agano la Mungu limeratibiwa vizuri na halitabadilika hivyo familia ya Daudi inaweza kuliamini.

Je yeye haongezi wokovu wangu... tamaa?

Daudi anaaamini kwamba Mungu atamsaidia daima na kumfanya afanikiwe.

2 Samuel 23:6

Maelezo ya Ujumla

Hii inahitimisha maneno ya mwisho ya Daudi.

Lakini yasiyofaa yote yatakuwa kama miiba na kutupwa mbali

Hapa waovu wanalinganishwa na miba isiyofaa.

kwa maana haiwezekani kukusanywa kwa mikono

"Kwa maana hakuna awezaye kuichukua kwa mikono yake bila kumwumiza"

Ni lazima yachomwe mahali yalipo

"Yalipo" ndipo yanapochomewa." Hii inamaanisha kwamba Mungu atawaharibu waovu.

2 Samuel 23:8

Yeshbaali

Hili ni jina la mwanamme. Matoleo mengine yanasomeka Yoshebu Bashebethi, Jashobeamu, Ishbaali, au Ishboshethi kwa hiyo nakala mbalimbali za kale zina tofauti hizi.

Mhakimoni

Hili ni jina la kundi la watu.

Mia nane

"800"

2 Samuel 23:9

Maelezo ya Ujumla

Hii inaendeleza orodha ya mashujaa wa Daudi.

Jeshi likarudi baada ya Eleaza

Hii inamaana jeshi lilirudi baada ya Eleaza kurudi kutoka vitani. Yaweza pia kuwa "Jeshi la Israeli lilirudi kwenye uwanja wa vita baada ya Eleaza kuwa ameshinda vita"

kwa ajili tu ya kuteka nyara miili

"Kuchua pekee walivyotaka katika maiti za maadui"

2 Samuel 23:11

Maelezo ya Ujumla

Hii inaendeleza orodha ya mashujaa wa Daudi

shamba la dengu

"katika shamba ambalo mtu alikuwa amepanda zao la dengu"

dengu

mbegu ya bapa, inaliwa kama maharage

jeshi lilikimbia

"jeshi la Waisraeli lilikimbia"

2 Samuel 23:13

Watatu kati ya thelathini

Hawa siyo askari waliotajwa katika 23:8

thelathini

"30" au "Askari thelathini wa Israeli waliokuwa mashujaa zaidi"

Pango la Adulamu

"Pango lililopo karibu na mji wa Adulamu." "Adulamu ipo karibu na Bethlehemu.

Bondel la Mrefai

Mrefai ni mtu aliyekuwa mmiliki wa bonde.

katika ngome yake

"katika eneo lake la ulinzi"

Wafilisiti wlikuwa wamejieneza katika Bethlehemu

"Baadhi ya askari wa Wafilisiti walikuwa wakimiliki kijiji cha Bethlehemu"

2 Samuel 23:15

kupita kati ya jeshi

"walipigania njia yao kupitia jeshi la adui"

Je ninywe damu ya watu waliohatilisha maisha yao?

Daudi analinganisha maji na damu kwa sababu wale watu walihatarisha maisha yao ili kuyalete kwake. Anatumia swali kusisitiza hili.

2 Samuel 23:18

Abishai ... Seruya.

Haya ni majina ya wanaume

kapteni juu ya watatu

Inamaana Abishai alikuwa kiongozi wa wale watatu walikwenda kumchukulia Daudi maji.

watu mia tatu

"watu 300"

alitajwa pamoja na wale askari watatu.

"Watu walimtaja walipozungumzia wale mashujaa zaidi watatu"

hakuwa maarufu zaidi ya wale watatu?

Swali linasisitiza jinsi alivyokuwa maarufu.

wale mashujaa watatu

Hii inarejerea kwa Yoshebu Bashebethi, Eleaza na Shama. Abishai hakuwa maarufu kama hawa askari hawa.

2 Samuel 23:20

Kabseeli

Hili ni jina la mji.

Yehoiyada

Hili ni jina la mwanamme.

Arieli

Hili ni jina la mwanamme.

2 Samuel 23:22

alifanya matendo haya

"alifanya matendo haya makuu"

naye alitajwa kati ya mashujaa watatu

"watu walimsifu kama wale mashujaa watatu"

Alikuwa na heshima kuliko mashujaa thelathini kwa ujumla wao, lakini hakuwa na heshima kama wale mashujaa watatu

"Alikuwa maarufu zaidi ya askari wale 30 isopokuwa wale watatu bora zaidi"

wale mashujaa zaidi watatu

Hii inamaanisha Yoshebu Bashebethi, Eleaza, na Shama.

mlinzi wake

Kundi la askari waliowajibika kumlinda Daudi

2 Samuel 23:24

Maelezo ya Ujumla

Hii ni orodha ya mashujaa wa Daudi

Thelathini

"Askari 30 maarufu zaidi"

2 Samuel 23:29

Maelezo ya Ujumla

Hii inaendeleza orodha ya mashujaa wa Daudi

2 Samuel 23:33

Maelezo ya Ujumla

Hii inaendeleza orodha ya mashujaa wa Daudi

2 Samuel 23:37

Maelezo ya Ujumla

Hii inahitimisha orodha ya mashujaa wa Daudi

Jumla yao thelathini na saba

jumla yao saba - "kulikuwa na 37 jumla yao"

2 Samuel 24

2 Samuel 24:1

Hasira ya Yahwe iliwaka juu ya Israeli

Neno "kuwaka" linamaanisha kuwasha moto. Hasira ya Yahwe inalinganishwa hapa na kule kuwasha moto

alimchochea Daudi kinyume chao

"alimfanya Daudi kuwapinga"

Nenda, wahesabu Israeli na Yuda

Katika sheria ya Musa, Mungu alizuia wafalme wa Israeli kuhesabu wapiganaji.

Dani hadi Beersheba

Kifungu kinatumia majina mawili, Dani kaskazini ya mbali na Bersheba, kusini ya mbali, kuwakilisha nchi nzima.

Hesabu watu wote... wanaofaa kwa vita

Hii inamaanisha wanaume wote isipokuwa walio watoto, wazee, au wasioweza kupigana kwa sababu ya udahifu wa miili yaoo.

2 Samuel 24:3

wazidishe... mara mia zaidi

Inamaanisha "kuzalisha watu mia moja kwa kila mtu aliyekuwepo wakati huo."

neno la mfalme lilikuwa la mwisho dhidi ya Yoabu

Yoabu na majemedari wengine wa Mfalme Daudi hawakufanikiwa kumshawishi Daudi kutochukua sensa.

neno la mfalme

Kifungu kinawakilisha agizo la mfalme juu yao.

2 Samuel 24:5

Walivuka

"Yoabu na majemedari wengine wa jeshi walivuka"

Aroeri

Huu ulikuwa mji katika ukingo wa Mto Arnoni.

Yazeri

Huu ni mji huko Gadi.

Tahitimu Hodshi

Huu waweza kuwa mji wa Kadehsi katika nchi ya Wahiti.

2 Samuel 24:8

walikuwa wameondoka

"Yoabu na majemedari walikuwa wameondoka"

miezi minane na siku ishirini

"miezi 9 na siku 20"

Ndipo Yoabu alipotoa taarifa ya hesabu kamili kwa mfalme kuhusu watu wawezao kupigana vita

Ndipo Yoabu alipomwambia mfalme jumla ya watu waliotayari kwa vita"

Katika Israeli

Hii inahusu makabila ya kaskazini mwa Israeli.

800,000... 500,000

"mia nane elfu... mia tano elfu"

wafutao upanga

Hii inamaanisha watu waliokuwa tiyari kwa vita jeshini.

wa Yuda

Hii inamaanisha kabila ya Yuda.

2 Samuel 24:10

moyo wa Daudi ukamchoma

"moyo" hapa unamaanisha hisia na dhamira ya Daudi.

Sasa, Yahwe, iondoe hatia ya mtumishi wako

Daudi anajitaja kama "mtumishi wako." Hii ni njia ya upole ya kuongea na mwenye mamlaka.

2 Samuel 24:11

neno la Yahwe likaja

Inamaanisha Yahwe aliongea. "Yahwe aliongea ujumbe wake."

neno la Yahwe

Hapa "neno" linawakilisha ujumbe wa Yahwe.

mwonaji wa Daudi

Hii inamaanisha Gadi alikuwa nabii wa ikulu.

2 Samuel 24:13

nipo katika shida kubwa

"nipo katika shida ya kutisha"

Haya na tuanguke katika mikono ya Yahwe kuliko kuanguka katika mikono ya mwanadamu

Hapa "mikono" inamaanisha mamlaka au umilki.

2 Samuel 24:15

muda uliopangwa

Huu ni muda Mungu aliokuwa amepanga kusitisha tauni.

elfu sabini

"70,000"

kutoka Dani hadi Beersheba

Hii inamaanisha taifa lote

6Malaika aliponyosha mkono wake kuelekea Yerusalemu ili kuuharibu

"mkono" unawakilisha nguvu ya malaika.

Yahwe akabadilisha nia yake kuhusu madhara

Inamaanisha Yahwe alisitisha baya alilokuwa amemruhusu malaika kufanya.

Basi rudisha mkono wako

"mkono" unamaanisha nguvu ya malaika.

Arauna

Hili ni jina la mwanamme

sakafu ya kupulia

Hii ilikuwa ni sehemu ngumu, iliyo na ubapa mahali nafaka zilikuwa zinapulwa.

2 Samuel 24:17

Nimetenda dhambi, na nimetenda kwa ukaidi

Hivi vifungu vinamaanisha kitu kimoja na vimetumika kwa msisitizo.

Lakini kondoo hawa, wamefanya nini?

Daudi anatumia swali na analinganisha watu na kondoo kusisitiza kwamba hawajakosa.

Tafadhari mkono wako uniadhibu mimi

Hapa "mkono" unamaanisha nguvu.

2 Samuel 24:18

kumsujudia mfalme uso wake mpaka juu ya ardhi

Alikuwa akionesha heshima kubwa kwa mfalme.

2 Samuel 24:21

ili tauni iondolewe miongoni mwa watu

"Ili kwamba Yahwe aiondoe tauni kutoka kwa watu"

Ulifanyie lolote lolote lililojema machoni pako

Kifungu "machoni pako" kinawakilisha wazo au oni la Daudi.

miganda ya kupuria

fito zilizotumika kupuria ngano.

2 Samuel 24:24

sitatoa chochote... nisichokigharimia

"Nitatoa tu kile nilichokilipia"

shekeli hamsini

"shekeli 50." Shekeli ni sawa na gramu 11.

badala ya nchi

Neno "nchi" linawakilisha watu wa Israeli.

1 Kings 1

1 Kings 1:1

walimfunika kwa nguo

Waliweka blanketi nyingi juu yake ili apate joto.

1 Kings 1:3

Kwa hiyo wakatafuta

"Kwa hiyo watumishi wa mfalme wakatafuta"

Katika mipaka yote ya Israeli

"katika nchi yote ya Israeli"

Abishaagi Mshunami

"Abishagi kutoka Shunami"

Mshunami

Mtu kutoka katika mji wa Shunami

mfalme

Mfalme Daudi

1 Kings 1:5

Adoniya mwana wa Hagithi

Hagithi alikuwa mke wa Daudi

alijiinua

"alianza kujivuna"

wapanda farasi

Watu wanaoendesha magari yanayovutwa na Farasi

magari na wapanda farasi hamsini ili wapige mbio mbele yake

Hawa watu walienda walitangulia mbele ya magari ili kuwaandalia njia na kuwalinda

alikuwa hajawahi mumsumbua, kwa kusema

"Alikuwa hajawahi kumsumbua. Alikuwa hajawahi hata kumwuliza" au "alikuwa hajawahi hata kutaka kumfanya awe na hasira, kwa hiyo hakuwahi hata kumwuliza"

Kwa nini umefanya hili na lile?

"Unapaswa kutambua kuwa kile ulichokifanya hakiko sawa."

aliyezaliwa baada ya Absalomu

Daudi alikuwa mzazi wa wote Absalomu na Adoniya, lakini walikuwa na mama zao tofauti. Absalomu alizaliwa, kisha Adoniya.

1 Kings 1:7

Akashauriana n a Yoabu

"Adoniya alijadili mipango yake na Yoabu"

Yoabu ... Seruya ... Abiathari ... Adonya ... Sadoki ... Benaya ... Yehoyada ... Nathani ... Shemei ... Rei

Mainaya wanaume

wakumfuata Adoniya

"wakamfauata na kumsaidia Adoniya" au "waliahidi kumsadia Adoniya"

1 Kings 1:9

ndama walionona

"ndama waliokuwa wamepewa chakula cha kutosha ili wanenepe" au "ng'ombe wachanga waliokuwa wameandaliwa kwa ajili ya sadaka"

jiwe la Sohelethi

Hili ni eneo lenye mwamba lililokaribu na Yerusalemu.

Eni Rogeli

Hili liliuwa jina la kisima ambacho watu walipata maji

ndugu zake wote, watoto wa mfalme

virai hivi viwili vinamaanisha kitu kilekile

wanaume wote wa Yuda, na watumishi wa mfalme

Virai hivi viwili vinamaanisha jambo lilelile.

1 Kings 1:11

Je, haujasikia kuwa ... hilo?

"unaonekana kuwa haujasikia ...hilo" au "Je, umesikia juu ... hilo?

Kuwa Adonya mwana wa Hagathi amekuwa mfalme

"Kwamba mwana wa Hagathi Adoniya amekuwa mfalme"

Hagathi

mama wa Adoniya na mke wa Dsudi.

1 Kings 1:13

Taarifa kwa ujumla

Nabii Nathani anendelea kuongea na Bathisheba

Je, haukumwapia mtumishi ... enzi?

"ulimwapia mtumishi wako ... enzi"

mtumishi wako

"kwangu, mtumishi wako"

ataketi kwenye kiti changu cha enzi

"atakuwa mfalme kama nilivyokuwa"

Kwa nini basi Adoniya anatawla?

"Kwa hiyo basi, Adoniya anapaswa kutokutawala"

kuthibitisha hayo

"mwambie kuwa hayo uliyosema ni ya kweli"

1 Kings 1:15

chumbani kwa mfalme

"chumba ambacho mfalme alilala"

Abishagi Mshunami

Tazama 1:3

akainama kifudifudi mbele ya mfalme

"akainama kuikaribia sakafu mbele ya mfalme"

una haja gani?

"unataka nikufanyie ini?"

ulimwapia mtumishi wako

Kiwakilishi cha "u" ni kinasisitiza kuwa "wewe mwenyewe uliapa"

mtumishi wako

Tazama 1:3

ataketi kwenye kiti changu cha enzi

Tazama 1:3

1 Kings 1:18

Taarifa kwa ujumla

Bathisheba anaendelea kuoongea na Daudi

Tazama

"Sikiliza kwa makini ninachotaka kukuambia"

Makaisai, ndama walionona,, na kondoo"

"makiisai wengi, ndama walionona na kondo wengi"

1 Kings 1:20

Taarifa kwa ujumla

Bathisheba anaendelea kuongea na Daudi

macho yote ya Israeli yako kwako

Neno "macho" liinamaanisha watu. "watu wote wa Israeli wanakutazama wewe"

atakayeketi kwenye kiti cha enzi

Tazama 1:13

wakati bwana wangu atakapolala na baba zake

"utakapolala na baba zako"

atakapolala na baba zake

Hii ni tafsida ya neno "kufa"

Mimi na mwanangu Sulemani kuhesabiwa wahaini

"Mfalme mpya atatuhesabu mimi na mwanangu Sulemani kuwa ni wahaini"

1 Kings 1:22

Taarifa kwa ujumla

Nabii Nthani anaongea na Daudi

akalala kifudifudi

"akasujudu chini sana"

1 Kings 1:24

Taarifa kwa ujumla

Nabii Nathani anaendelea kuongea na Daudi

ataketi kwenye kiti changu cha enzi

Tazama 1:3

wanakula na kunywa

"wanankula na kunywa pamoja naye"

1 Kings 1:26

Taarifa kwa ujumla

Nabii Nthani anandea kuongea na Daudi

bwana wangu mfalme

Nathani anaongea na Daudi kana kwamba mfalme Daudi ni mtu mwingine ili kuonesha heshima kwa Daudi

ataketi kwenye kiti changucha enzi

Tazama 1:13

1 Kings 1:28

Taarifa kwa ujumla

Mfalme Daudi anamwahidi Bathisheba

akaja akasimama mbele ya mfalme

"akaja mbele ya mfalme" au "akarudi kwa mfalme"

akafanya kiapo

"akafanya ahadi "

atakayeketi kwenye kiti changu cha enzi

Tazama 1:13

Bwana wangu mfalme Daudi na aishi milele

Bathisheba alijua kuwa Daudi hataishi milele, hii ni namna ya kusema kuwa Daudi ni mfalme mwema.

1 Kings 1:32

Taarifa kwa ujumla

Daudi anampaka mafuta Sulemani kuwa mfalme

uwachukue watumishi wangu

"watumishi wangu"

Gihoni

Hilini jiina la kisima

1 Kings 1:35

Taarifa kwa ujumla

Mfalme Daudi anaendelea kuongea kwa niaba ya Sulemani kuwa yeye ndiye atakayekuwa mfalme

atakuja kukaa kwenye kiti changu

Tazama 1:13

Na iwe hivyo

Walikubali na kufanya kama vile mfalme Daudi alivyosema

BWANA, Mungu wa mafalme bwana wangu, alithibitishe hilo

"Bwana wangu mfalme, BWANA, Mungu wako na alithibitishe"

alivyokuwana mfalme bwana wangu

"amekuwa na wewe, bwana wangu mfalme, kwa hiyo"

na kuifanya enzi yake kuwa kubwa kuliko enzi ya bwana wangu Daudi.

neno "enzi" linamaanisha 1) mtu anayekaa kwenye kiti cha enzi. "kumfanya yule anayekaa kwenye kiti cha enzi kuwa mkubwa kuliko bwana wangu Daudi" au 2) ufalme ambao yule aketiye kwenye kiti cha enzi anatawala, au "kuufanya ufame wake kuwa mkubwa kuliko ufame wa bwana wangu Daudi"

enzi ya bwana wangu Daudi

"enzi yako, bwana wangu mfalme Daudi"

1 Kings 1:38

Taarifa kwa ujumla

Watu wa Israeli wanampaka mafuta Sulemani kuwa mfalme wa Israeli.

Wakerethi ... Wapelethi

majina ya makundi ya watu

Gihoni

jina la kisima, mahali ambapo maji baridi hutoka katikta ardhi

akachukua pembe lenye mafuta hemani

alichukua pemba maalumu la mnyama lililokuwa limejaa mafuta ya mizeituni ambayo makuhani walikuwa wameyatunza kwenye hema maalumu ya BWANA.

pembe ya mafuta

Hii inaweza kumaanisha 1) pembe ya mnyama iliyojaa mafuta ya mizeiituni au 2) choombo ambacho kilitumika badala ya pembe lakini watu bado waliendelea kuita pembe, "chombo cha mafuta"

1 Kings 1:41

Taarifa kwa ujumla

Adoniya anasikia kelele na anasubiri habari.

1 Kings 1:43

Taarifa kwa ujumla

Adoniya anagundua kuwa Sulemani ndiye mfalme mpya

Wakerethi ... Wapelethi

majina ya makundi ya watu.

1 Kings 1:46

Taarifa kwa ujumla

Yonathani anaenedelea kumwambia Adoniya juu ya Sulemani

amaeketi kwenye kiti cha enzi cha ufalme

Tazama 1:35

mtu kuketi kwenye enzi yangu

Tazama 1:35

1 Kings 1:49

Taarifs kwa ujumla

Adoniya anamwogopa mfalme Sulemani

Wakasimama

"Walianza kufanya mabo yao haraka"

Adoniya ... akasimama kisha

"Adoniya kwa haraka"

Adoniya ... akachukua pembe la madhabahuni

"pembe la madhabahuni" inaonyesha ulinzi wa BWANA.

amemwogopa mfalme Sulemani

"anakuogopa, Mfalame Sulemani"

hatamwua mtumishi wake

"hataniua"

1 Kings 1:52

Taarifa kwa ujumla

Sulemani anaghairi kumwua Adoniya

hakunahata unywele mmoja utakaoanguka

"Nitamlinda awe sakama"

uovu utaonekana kwake

"atakapofanya uovu"

1 Kings 2

1 Kings 2:1

Mimi sas ninnaiendea njia ya dunia yote

Hii ni tafsida ya kusema "Mimi naelekea kufa"

ujionyeshe mwenyewe kama mwanamume

"Mwonyeshe kila mmoja kuwa wewe ni mwanamume" au ":uishi maisha ambayo kila mmoja atakuona kuwa wewe ni mwanamume mwema"

ukitembea katika njia zake

"uishi maisha anayokuamuru"

ufanikiwe

"kufanikisha" au "kufanya vizuri"

atayatimiza maneno yake

"atafanya kila kitu alichoahidi kufanya"

kama wanao ... hawatakoma

BWANAanamwambia Daudi, kwa hiyo maneno "o" na "wa" yanamwakilisha Daudi.

wakatembea mbele yangu kwa uaminifu

BWANA anamwabia Daudi. kwa hiyo neno "yangu" linamwakilisha BWANA.

kwa mioyo yao yote na kwa roho zao zote

kujitoa kikamilifu

hawatakoma kuwa na mtu katika kiti cha enzi cha Israeli

"Mmoja wa wana wa kizazi chako ataendelea kuwa mfalme."

1 Kings 2:5

Taarifa kwa ujumla

Mfalme Daudi anaendelea kumwambia Sulemani jinsi ya kuingoza Israeli.

kile Yoabu ...alichonifanyia, na kike alichowafanyia

Dudi anamaanisha kitu kilekile mara mbili. "kile Yoabu ... alichonifanyia, hiyo maanisha,kile alichofanya"

alimwaga damu vitani wakati wa amani

Yaweza kumaanisha 1) "aliwaua wale wanaume wakati wa amani kama vile ilikuwa wakati wa vita" au 2) "aliwalipizia kisasi wale wanaume wakati wa amani kwa sababu walikuwa wameuwa watu vitani"

na kuiweka ile damu kwenye mshipi na kwenye vie viatu miguuni mwake

Yoabu alikuwa karibu sana na wale wanaume wakati alipokuwa akiuwaua kiasi kwamba damu yao ilirukia kwenye mshipi wake na kwenye viatu vyake.

viatu

kile ambacho watu huvaa miguuni

usiache mvi zake ziingie kaburini kwa amani

"hakikisha Yoabu anakufa kifo cha kuuawa kabla hajazeeka."

1 Kings 2:7

Taarifa kwa ujumla

Mfalme Daudi anaendelea kumwambia Sulemani jinsi ya kuingoza Israeli.

Barizilai

jiina la mwanamume

uwaache wawe miongoni mwa wale wanaokula mezani mwako

"uwakaribishe kula mezani kwako"

1 Kings 2:8

Taarifa kwa ujumla

Mfalme Daudi anaendelea kumwambia Sulemani jinsi ya kuingoza Israeli.

Shimei ... Gera

Haya nimajina ya wanaume

Wabenjamini

Wana wa uzao wa Benjamini

Bahurimu ... Mahanaimu

Majina ya mahali

usimwache aiepuke adhabu

"hakikisha unamwadahibu

Uatkileta hicho kichwa chenye mvi kaburini

"hakikisha anakufa kifo cha kuuawa"

1 Kings 2:10

Taarifa kwa ujumla

Daudi anakufa na Sulemani anakuwa mfalme mpya wa Israeli.

alipolala na mababu zake

"alipokufa"

Daudi ... na alizikwa

"Daudi ... na wakamzika"

Siku ambazo Daudi alitawala Israeli zilikuwa ni

"Muda ambao Daudi alitawala Israeli walikuwa" au "Daudi alitawala Israeli kwa muda wa "

akaketi kwenye kiti cha enzi cha baba yake Daudi

"kiti cha enzi kinawakilisha mamlaka ya mfalme

akaketi kwenye kiti cha babayake Daudi

"akawa mfalme, kama vile Daudi baba yake alivyokuwa"

1 Kings 2:13

Taarifa kwa ujumla

Adoniya anakuja kuongea na Bathisheba

kwa amani

"bila kuwa na kusudio la kusababisha maumivu"

mambo yamebadilika

"Kile kilichokusudiwa kutokea hakikutokea"

ufalme umegeuzwa na umekuwa wa ndugu yangu

"BWANA alimpatia ufalme ndugu yangu" au "ndugu yangu amekuwa mfalme"

1 Kings 2:16

Taarifa kwa ujumla

Adoniya anamshirikisha Bathisheba ombi lake

Usinikatalie ... hatakukatalia

"Tafaadhali fanya kama ninavyofanya ... kwa hakika atafanya kama unavyosema"

Abishagi Mshunami

Tazama 1:3

1 Kings 2:19

Taarifa kwa ujumla

Bathisheba anaenda kwa mfalme Sulemani akiwa na ombi la Adoniya

kiti kingine cha enzi kilicholetwa

"alimwagiza mtu kuleta kiti cha enzi

sitakukatalia

"Nitakupa utakachoomba"

1 Kings 2:22

Taarifa kwa ujumla

Mfalme Sulemani anatoa jibu la ombi la Adoniya

Kwa nini unamwombea ... Adoniya? Kwa nini usimwombea na ufalme pia ... Sruya?

"Umekosea kumwombea ... Adoniya! Hii ni sawa na kumwombea ufalme pia ... Seruya!" au "Nadhani nimruhusu kuwa mtawala wa ufalme pia!"

Mungu wangu na anifanyie hivyo, na zaidi pia, k ama Adoniya hajayasema hayo kinyume na maisha yake

Mungu atakuwa na haki zote za kuniua na hata kunifanyia hata mabaya zaidi kama sitamwuwa Adoniya kwa sababu ametoa ombi hili"

1 Kings 2:24

Taarifa kwa ujumla

Mfalme Sulemani anamwua Adoniya

na kunipa kiti cha enzi

"Neno "kiti cha enzi" linamaanisha mamlaka ya Sulemani ya muwa mtawala kama alivyokuwa amepewa na BWANA.

ambaye amenifanyia nyumba

Neno "nyumba" linamaanisha uzao ambao Mungu alikuwa amempa mfalme Sulemani, ambao utaendelea kutawala baada ya Yake.

1 Kings 2:26

Taarifa kwa ujumla

Abiatahari amefukuzwsa kwenye ukuhani na mfalme Sulemani.

na kujitaabisha kwa namna mbalimbali kama baba yangu alivyopata tabu

Abiathari alijitabisha pamoja na mfalme Daudi kabla Daudi hajawa mfalme.

ili kwamba atimilize

Neno "a" linamwakilisha mfalme Sulemani

alivyokuwa amesema

neno "a" linamwakilisha BWANA

1 Kings 2:28

Taarifa kwa ujumla

Mfalme Sulemani anamwagiza Benaya kumwusa Yoabu

Habari hizo zikamfikia Yoabu

"Yaabu akasikia kile ambacho Sulemani alifanya baada ya kuwa mfalme"

pembe za madhabahuni

pembe za madhabahuni zinamaanisha mamlaka ya BWANA na ulinzi.

1 Kings 2:30

Taarifa kwa ujumla

Benaya anaenda kumwua Yoabu

uitoe kwangu na kwenye nyumba ya baba yangu damu ambayo Yoabu alimwaga bila sababu

"uiondoe hatia ya mauaji ambayo Yoabu aliyafanya kutoka kwangu na familia yangu"

1 Kings 2:32

Taarifa kwa ujumla

Mfalme Sulemani anaeleza sababu ya Yoabu kuuawa

BWANA na amrudishie damu yake kichwani mwake

"Neno "mwake" linamaanisha Yoabu. "Damu" linamaanisha hatia.

wasio na hatia na wema kuliko yeye

Maneno haya mawili yanamaanisha kitu kilekile na yanatia msisitizo kuwa Abineri na Amasa walikuwa wanaume wema kuliko Yoabu.

Yoabu kichwani pake na kwenye kichwa cha uzao wake

Neno "kichwa " linatumika kumaanisha mtu kamili

na nyumba yak,e na kwenye kiti chake cha enzi

Neno "nyumba" na "kiti cha enzi" linamaanisha uzao wa Daudi na utawala wa Daudi."

1 Kings 2:34

Taarifa kwa ujumla

Benaya anamwua Yoabu na anakuwa na akuwa mkuu wa jeshi la mfalme Sulemani

Alizikwa kwenye nyumba yake

"Yoabu alizikwa kwenye nyumba yakae

1 Kings 2:36

Taarifa wa ujumla

Mfalme Sulemani anamwambia Shimei kubaki Yerusalemu vinginevyo atakufa

Damu yako itakuwa juuy a kichwa chako

Neno "damu: linawakilisha hatia.

1 Kings 2:39

Taarifa kwa ujumla

Shimei anaondoka Yerusalemu

Akishi ... Maaka ... Gathi

Akishi na Maaka nii majina ya wanaume; Gathi ni jina lamji wa Filisti

1 Kings 2:41

Taarifa kwa ujumla

Mfalme Sulemani anamhukumu Shimei kwa kuondoka Yerusalemu

Je, sikukuapisha ... nikisema, Tambua ...utakufa?

"Unatambua vizuri sana kuwa nilikuapisha ...Nikisema, 'Tambua ... utakufa'!"

1 Kings 2:43

Taarifa kwa ujumla

Mfalme Sulemani anatoa hukumu juu ya Shimei kwa sababu ya kuondoka Yerusalemu.

Kwa nini basi umeshindwa kulinda kiapo chako ... nuliyokupa?

Inaweza kumaanisha 1) Sulemani anataka kjua jibu au 2)"umefanya makosa kwa kuvunja kiapo chako ... wewe"

kichwani pako

Neno "kichwa" linamaanisha mtu kamili. "juu yako"

1 Kings 2:45

Taarifa kwa ujumla

Mfalme Sulemani anatoamari ya kumwua Shimei

na enzi ya Daudi itaimrika mbele ya BWANA milele

Neno "enzi ya Daudi" linamaanisha mamlaka na utawala wa Daudi na uzao wake wote milele.

Kwa mkono wa Sulemani

matumizi ya "mkono" unawakilisha nguvu ya Sulemani

1 Kings 3

1 Kings 3:1

Taarifa kwa ujumla

Sulemani anamwoa mwanamke wa Kimisri

Sulemani akawa na ushirikiiano ... na Farao mfalme wa Misri

Sulemani anaanzisha uhusiano na Farao

nyumba ya BWANA

"hekalu"

mahali pa juu

"mahali ambapo watu huabudu na kufanya makafara kwa miungu"

1 Kings 3:4

Taarifa kwa ujumla

Mungu anamwuliza Sulemani kuwa amfanyie nini:

eneo kuu la juu

"eneo linalofahamika sana kwa kutolea kafara" au "madahabu ya muhimu sana"

Omba! unataka nikupe nini?

"Niombe unalotaka nami nitakupa" au "Unataka nini?

1 Kings 3:6

Taarifa kwa ujumla

Sulemani anajibu swali la Mungu

Umeonesha uaminifu wa agano mkuu

"Umekuwa mwaminifu kwa makubaliano yako"

kwa sababu alitembea mbele yako kwa ukweli na uaminifu, katika haki ya moyo

"kwa sababu alikuwa mwaminifu, mwenye haki na mkweli"

kuketi kwenye kiti chake cha enzi

"kutawala mahali pake"

1 Kings 3:7

Taarifa kwa ujumla

Sulemani anaomba hekima

Mimi ni mtoto mdogo

Sulemani anasema kuwea yeye ni kama mtoto mdogo ambaye hajui kama baba yake anavyojua.

Sijui namna ya kuingia na kutoka

"Sijui njia sahihi ya kufikiri" au "Sijui namna ya kuwa mfalme"

Kwani ni nani awezaye kuwahukumu watu watu wako hawa walio wengi?

Sulemani anauliza swali ambalo jibu lake liko wazi. Jibu lake ni kwamba "hakuna awezaye." "Hakuuna awezaye kuwahukumuhawa watu wako wakuu"."

1 Kings 3:10

Taarifa kwa ujumla

Munga anampatia Sulelmani hekima na vitu vingine.

uhai wa adui zako

Sulemai hakumwamba Mingu ampe uwezo dhidi ya adui zake. "adui zako wauawe" au "uwezo wa kuwaua adui zako"

Tazama sasa nitafanya yote uliyoomba wakati uliponipa ombi lako

"Nitafanya kile ulichoomba nifanye pale uliposema nami"

1 Kings 3:13

kama utataembea katika njia zangu na kuyatunza maagizo

"kuishi kama nianvyotaka na ktii"

nitakapoziongeza siku zako

"siku" linamaanisha siku za Sulemani. "nitakufanya uishi maisha marefu"

1 Kings 3:15

ndoto

Ndoto ni kitu ambacho huwapata watu katika akili zao wanapokuwa katika usingizi. Hutokea na watu wakaona kama ni katu halisi na kumbe sivyo. Wakati mwingine Mungu hutumia ndoto kufikisha ujumbe kwa watu wake.

Yerusalemu

Kwa asili Yerusalmu ulikuwa mji wa Wakanaani ambao b aadaye ulikuja kuwa mji wa muhimu wa Israeli. Mjihuu uko kilomita 34 magharibi mwa bahari ya chumvi na kaskazini kidogo mwa Bethelehemu. Mpaka sasa bado ni mji mkuu wa Israeli.

sanduku la agano la Bwana, sanduku laamri ya agano, sanduku la BWANA

sentensi hizi zinamaanisha sanduku maalumu ambalo limesakafiwa kwa dhahabu, ambalo ndani mwake kulikuwa na vile vidonge viwili vya mawe vilivyokuwa vimeandikwa amri kumi za Mungu. Pia lilikuwa na fimbo ya Haruni pamoja na jagi la mana.

Bwana

Neno "Bwana" linamaanisha mtu aliye naumiliki fulani pia mwenye mamlaka juu ya watu. Lina hili linapoanza kwa herufi kubwa humaanisha Mungu.

sadaka za kuteketezwa, sadaka za moto

sadaka za kuteketezwa zilikuwa ni aina za sadaka ambazo zilikuwa zimechomwa kwa moto madhabahuni. Zilitengenezwa kwa ajili ya fidia ya dhambi za watu. Sadaka hizi zilijulikana pia kama "sadakaza moto."

sadaka za amani

"sadaka za amani" zilikuwa ni moja kati ya sadaka nyingi ambazo Mungu aliwaamuru Waisraeli kutoa. Pia ziliitwa "sadaka za shukurani" au "sadaka za amani"

sherehe

Neno "sherehe" linamaanisha tukio ambalo makundi ya watu walikula chakula kingi kwa pamoja kwa lengo la kufurahia jambo fulani. Wakati mwingine kunakuwa na chakula maalumu.

mtumishi, mtumwa, utumwa

Neno "mtumishi" linaweza kumaanisha "mtumwa" lenye maana ya mtu anayetumika kwa mtu mwingine kwa kupenda yeye au kwa kulazimishwa.

1 Kings 3:16

Taarifa kwa ujumla

Makahaba wawili wanamwomba Sulemani awaamue

1 Kings 3:18

Taarifa kwa ujumla

Wale makahaba wawili wanamsimulia Sulemani kisa chao

alimlalia

"kwa bahati mbaya alijigeuza juu ya yule mt

1 Kings 3:21

Taarifa kwa ujumla

Makahaba wawili wanaendelea kumweleza kisa chao Sulemani

kumhudumia mwanangu

Hii inamaanisha kumnyonyesha mtoto kwa maziwa yake.

mbele ya mfalme

"mbele ya Sulemani"

1 Kings 3:23

Taarifa kwa ujumla

Sulemani anafanya uamuzi kwa wale wanawake wawili.

1 Kings 3:26

Taarifa kwa ujumla

Yule mama halisi wa yule mtoto anamwomba mfalme asimwue yule mtoto.

moyo wake ulikuwa na huruma sana kwa mwanae

"alimpenda sana mtoto wake"

1 Kings 4

1 Kings 4:1

Taarifa kwa ujumla

wakuu wa ofisi ya Sulemani

Azaria ... Sadoki ... Elihorefu ... Ahiya ... Shisha ... Yehoshafati ... Ahiludi .. Benaya ... Yehoyaida ... Abiathari

Haya yote ni majina ya wanaume

1 Kings 4:5

Taarifa kwa ujumla

Wakuu wengine wa Ofisi ya Sulemani

Azaria ... Nathani ... Zabudi ... Adoniramu ... Abda

Haya yote ni majina ya wanaume

1 Kings 4:7

Taarifa kwa ujumla

Mwendelezowa wakuu wa ofisi ya Sulemani

Beni Huri ... Beni Dekeri ... Beni Hesedi

Haya ni majina ya wanaume. Neno "Beni" nyuma ya jina inamaanisha "mwana wa" kwa hyo "Beni Huri" inamaanisha "mwana wa Huri."

Efraimu ... Makazi ... Shaalibimu ... Bethi Shemeshi ... Elonbethi Hanani ... Arubothi ... Sokohi Hefa

Haya ni majina ya mahali

1 Kings 4:11

Sentensi unganishi

Mwendelezo wa wakuu wa ofisi ya Sulemani

Beni Abinadabu ... Beni Geberi ... Yairi ... Manase ... Ahinadabu ... Ido

Haya ni majina ya wanaume

Tafathi

Hili ni jina la mwanamke

Dori ... Bethi Shani ... Zarethani ... Yezreeli ... Bethi Shani hadi Abeli Mehola ... Jokimeamu ... Ramothi Gileadi ... Arigobu ... Bashani ... Mahanaimu

Haya ni majina ya mahali

1 Kings 4:15

Taarifa kwa ujumla

Mwenedelezo wa wakuu wa ofisi ya Sulemani

Ahimaazi

Yeye alikuwa anatoka kabila la Naftali na laimwoa Basemathi

Baana

Baba yake, Husahi, alikuwa anatoka kabila ya Asheri na alimwoa Bealothi.

Yehoshafati

Baba yake, Parua, alikuwa anatoka kabila ya Isakari.

1 Kings 4:18

Taarifa kwa ujumla

Mwenedelezo wa wakuu wa ofisi ya Sulemani

katikanchi

Neno "nchi" linamaanisha nchi ya Yuda; wale wakuu wa ofifi ya Sulemani walikuwa wanatoka sehemu mbalimabli za Israeli

1 Kings 4:20

wengi kama mchanga wa bahariini

Hii ni lugha ya umbo

Mto

"Mto Frati"

Nchi ya Wafilisti

Eneo walimoishi Wafilisti

Kori thelathini

Kori moja kilikuwa kipimo cha mzigo mmoja

ayala, paa, na kulungu

"hawa ni aina ya ayala"

1 Kings 4:24

Tifsa

Hili ni eneoambalo leoliko Kaskazini mashariki mwa Ashuru

Yuda na Israeli

Majinaya Yuda na Israeli hutumika kumaanisha watu wa Israeli na wa Yuda.

kila mtu chini ya mzabibu wake na chini ya mtini wake

"kilafamilia ilikuwa na bustani yake ya mizabibu na mitini," ahaii inamaanisha kuwa watu waliishi kwa amani kwa sababu hawakuishi wakati wa vita na hivyo walikuwa na muda kwa ajili ya kufanya shughuli za bustanini.

Kutoka Dani mpaka Bereerisheba

Hii inamaanisha nchi yote ya Israeli kwa maana ya kutokaDani ambako ni kaskazinihadi Beerisheba ambako ni kusini.

1 Kings 4:26

mabanda ya farasi

Banda ni mahali ambapo hukaa wanyama kama vile punda

Walihakikisha hakuna kilichopungua

"walitoa kila kitu ambacho Sulemani alihitaji"

1 Kings 4:29

ufahamu na upana wa kuelewa kama mchanga wa baharini

Ule ukubwa wa uelewa wa Sulemani umefananishwa na mchcanfa wa baharini, ambao kimsingi hakuna awezaye kuuhesabu

watu wote wa mashariki

Hii inamaanisha nchi zilizokuwa mashariki mwa nchi ya Israeli kama vile Arabia na Mesopotamia.

Etheni ... Hemani ... Kaliko Darda... Maholi

Haya ni majina ya wanaume

1 Kings 4:32

Mierezi ... Hisopo

Majina ya miti

1 Kings 5

1 Kings 5:1

Taarifa kwa ujumla

Sulemani anaongea na mfalme Hiramu juu ya ujenzi wa hekalu

kwani Hiramu alimpenda Daudi

"kwa kuwa Hiramu alikuwa rafiki wa karibu wa Daudi"

kwa kuwa wakati wa uhai wake BWANA alikuwa akiwaweka adui zake chini ya nyayo za miguu yake

"BWANA alikuwa akimsadia Daudi kuwashinda adui zake" au"Daudi alikuwa na majukumu mengi kwa kuwa BWANA alikuwa akimpatia ushindi dhidi ya adui zake."

kujenga nyumba kwa jina la BWANA

"kujenga hekalu ambalo kwalo tutamwabudu BWANA"

1 Kings 5:4

Taarifa kwa ujumla

Sulemani anaendelea kuongea na mfalme Hiramu juu ya ujenzi wa hekalu

amenipa mimi pumziko toka pande zote

wakati wamfalme Daudi natu wa Israeli kulikuwa na vita, lakini sasa mafalme Sulemani na watu walikuwa na pumziko na amani.

nitamweka kwenye kiti chako cha enzi

"nitamfanya kuwa mfalme baada yako"

1 Kings 5:6

Taarifa kwa ujumla

Sulemani anaendelea kuongea na mfalme Hiramu juu ya ujenziwa hekalu

Lebanoni

Mfalme Hiramu alikuwa mfalme wa mji wa Tiro, ambao ulikuwa kwenye eneo hilohilo ambalo kwa leo linaitwa Lebanoni

Hakuna mtu miongoni mwetu anayejua kukata miti kama Wasidoni

"Wafanya kazi wako wanajua kukati miti kuliko watu wangu"

Wasidoni

"Watu wa Sidoni"

1 Kings 5:7

Taarifa kwa ujumla

mfalme Hiramu anamjibu Sulemani

maneno ya Sulemani

"Kile ambacho Sulemani alisema"

BWANA na abarikiwe leo

"Ninamsifu BWANA leo"

Mierezi

Mierezi ni aina fulani ya miti ambayo itatumika katika ujenzi wa hekalu

1 Kings 5:9

Taarifa kwa uumla

Mfalme Hiramu anaendelea kumjibu Hiramu

nami nitaileta katika makundi

"kuifunga kwa pamoja ili iweze kuelea kwa makundi

Nitaigawa pale

"nitayafungua hayo makundi ya miti"

Utafanya kile ninachohitaji

"Unaweza kufanya kile ninachotaka" au " unaweza kunilipa"

1 Kings 5:10

Miberoshi

Neno "Miberoshi" linamaanisha aina nyingi ya miti ikiwemo mierezi

Kori za ngano

Hiki kilikuwa kipimo cha vitu vikavu ambapo mafuta ndiyo yaliyokuwa kipimo cha kimiminika.

mwaka kwa mwaka

"kila mwaka"

1 Kings 5:13

Taarifa kwa ujumla

Sulemani anawashurutisha watu kujenga hekalu

akaandaa wafanyakazi kutoka Israeli yote

"akawashurutisha toka Israeli yote"

kwa zamu

Wafanyakazihawakwenda wote kwa pamoja; makundi yalienda moja baada ya lingine ili kushirikiana katika kazi.

Kwa mwezi mmoja walienda Lebanoni na miezi miwili walikaa nyumbani

Kila yale makundi matatu walitumia mwezi mmoja wakifanya kazi Lebanoni na kisha walikaa miezi miwili nyumbani Israeli.

1 Kings 5:15

Taarifa kwa ujumla

Sulemani anaendelea kuwashurutisha watu kujenga hekalu

mizigo

"vitu vizito"

wakata mawe milimani

"wanaume waliochimba mawe kutoka ardhini na kuyachonga"

1 Kings 5:17

Taarifa kwa ujumla

Sulemani anaendelea kuwashururtisha watu kujenga hekalu

walileta mawe makubwa ya thamani

"walichimba mawe mazuri kutoka mlimani n a kuyachonga katika sura takiwa"

Wagebaliti

"Hawa ni wanaume toka mji wa Gebali" Gebali ulikuwa mji uliokuwa mlimani karibu na Tiro huko Lebanoni.

1 Kings 6

1 Kings 6:1

Taarifa kwa ujumla

Maandiko yanaorodhesha vipimo vya hekalu

Sulemani akaanza kujenga

Sulemani hakujenga pekee yake; watumishi wake ndio waioifanya hiyo kazi

wa 480 ... wa nne

wa 480 ... wa4

katika mwezi wa Zivi, ambao ndio mwezi wa pili

"Zivi" ni jiina la mwezi wa pili wa kalenda ya Kihebrania. Mwezi huu uko kati ya sehemu ya mwisho wa mwezi wa Aprili na mwanzo wa sehemu ya mwezi Meyi wa kalenda ya Kimagharibi.

dhiraa

Dhiraa moja ni sawa na sentimenta 46

1 Kings 6:3

Taarifa kwa ujumla

Maandiko yanaorodhesha vipimo vya hekalu

ukumbi

ni sehemu ya jengo yenye safu na paa inayoonyesha uelekeo na kuunganisha jengo na sehemu ya mlango kuingilia.

1 Kings 6:5

Taarifa kwa ujumla

Maandiko yanaorodhesha vipimo vya hekalu

Kile chumba cha chini ... cha kati ... cha tatu

Hii inaonyesha vyumba vya kila sehemu ya jengo

Aupande wa nje akaupunguza upande wa nyumba

Walitengeneza kuta kuzunguka jengo ili kuzilinda nguzo za vyumba vidogovidogo

boriti

Hiki ni kipande kirefu na kizito cha ubao unaotenengenezwa ili kulinda jengo.

1 Kings 6:7

nyumba

Neno "nyumba" limetumika kumaanisha nyumba ya Mungu, hekalu

mawe yaliyokuwa yamechongwa chimboni

Chimo ni sehemu ambayo mawe makubwayalikuwa yakichimbwa huko mlimani na kuchongwa kwa vifaa ili kuyalainisha. Mawe yaliandaliwa chimboni na kuletwa hekaluni.

1 Kings 6:9

Sulemani akalijenga hekalu akalimaliza

Sulemai ahakulijenga hekalu pekee yake; watumishi wake ndio walioifanya hiyo kazi

Akavijenga na vyumba vya pembeni

Hivi ni vyumba vilevile ambavy ovimeonyeshwa kwenye jengo.

kwa boriti na mbao za mwerezi

boriti ni kipande kirefu na kizito cha ubao unaotengenezwa ili kulinda jengo. Papi ni kipande cha mti uliobapa ambao pia hutumika katika ujenzi.

vyumba vya ndani

"kuta za ndani"

mbao za mierezi

Neno "mbao" ni neno la jumla ambalo linatumika kuonesha ubao unaotumika kwa kujengea, kama vile boriti na papi

1 Kings 6:11

Neno la BWANA

"BWANA alinena ujumbe wake"

Nno la BWANA

Hapa "neno" linawakailisha ujumbe wa BWANA.

utatembea katika maagizo yangu

"utaendelea kutii maagizo yangu yote"

kuhukumu kwa haki

kutii na kufuata sheria za Mungu

kutunza amri zangu na kuishi kwa hizo

"kuwa mwangalifu na kufanya kila kitu nilichokuambia"

nitakapozithibitisha ahadi zangu

Muungu atazithibitisha ahadi zake kwa kutimiza kile alichoahidi kufanya.

Nitaishi

"Roho yangu itakaa hekaluni"

1 Kings 6:14

Sulemani

"wafanya kazi wa Sulemani"

za ndani

"ndani"

mierezi

mierezi ni aina ya miti iliyotumika kujenga hekalu

1 Kings 6:16

Dhiraa

Dhiraa moja ni kama sentimita 46

ukumbi mkuu

"chumba kikuu"

vibuyu

ni aina ya mboga za majani zenye umbo la duara ambazo hupandwa kwenye mizabibu

maua yaliyochanua

"maua yaliyofunguka"

1 Kings 6:19

madhabahu aliifunika kwa mbao za mierezi

Madhabau ilitumika kwa kuchoma ubani

1 Kings 6:21

Akaisakafia

"aliifunika"

madhabahu yote ya chumba cha ndani

"madhabahu ya uvumba iliyokuwa kwenye lango la kuingia chumba cha ndani"

1 Kings 6:23

mbao za mizeituni"

mbao zinazotokana na miti ya mizeituni

bawa mojahadi jingine

umbali uliokuwepo toka bawa moja hadi jingine

vipimo

"kiasi cha ukubwa"

1 Kings 6:27

Sulemani aliliweka ... Sulemani aliwafunika

"Sulemani" kwa maneno haya inamaanisha wafanyakazi wake

chumba cha ndani kabisa

jina jingine la patakatifu sana

aliwafunika

"alisakafia"

1 Kings 6:29

sura

umbo

1 Kings 6:31

Sulemani akatengeneza

"Wafanyakazi wa Sulemani walitengeneza"

vizingiti

sehemu ya juu inayoshikilia miimo ya mlango

kwenye pande tano

mashikio yaliyo katika pande za milango

Akasakafia

"akafunika"

1 Kings 6:33

Kwa njia hii, akalitengenezea hekalu miimo

Sulemani alitengeneza pia miimo kwenye lango la hekalu

yenye pande

yenye mashikio

Zile mbao mbili za mlanago mmoja

Inamaanisha kuwa kila mlango ulikuwa na sehemu mbilia ambazo zilikuwa zimefungwa pamoja.

1 Kings 6:36

Akalijenga korido la ndani

"Sulemani alizijenga kuta za korido la ndani" au "wafanya kazi wa Sulemani wakazijenga kuta za korido la ndani"

mihimili ya mierezi

Hizi ni mbao kubwakubwa za mierezi ambazo ziliwekwa kwa ajili ya kulinda kuta

1 Kings 6:37

mwaka wa nne ... mwaka wa kumi na moja

Hii ni miaka inayohesabiwa tangu Sulemani alipokuwa mfalme

Nyumba ya BWANA

"hekalu"

katika mwezi wa Ziv

Tazama 6:1

Katika mwezi wa Buli

"Buli" ni mwezi wa nane wa kalenda Kihebrania. Mwezi huu uko katika ya sehemu ya mwezi Oktoba na sehemu ya kwanza ya mwezi wa Novemba.

1 Kings 7

1 Kings 7:1

Taarifa kwa ujumla

Mwandishi anaandika juu ya ikulu ya Sulemani

Iliimchukua Sulemani miaka kumi na tatu kujenga ikulu yake

Kwa Sulemani alikuwa mfalme, wafanyakazi wake walifanya kazi kwa niaba yake.

ikulu yake

nyumba ya utawala

ikulu iliyoitwa mwitu wa Lebanoni

nyumba ya mwitu wa Lebanoni

Dhiraa

kiasi cha sentimita 46

mihimili

Hizi ni mbao kubwakubwa za mierezi ambazo ziliwekwa kwa ajili ya kulinda paa

1 Kings 7:3

Taarifa kwa ujumla

Baadhi ya taarifa ziinazohusu jengo la ikulu zinatolewa.

Paa la ikulu lilezekwa kwa mierezi

"kuliwekwa mihimili ya mierezi kwa lengo la kulinda paa"

mihimili

Hizi ni mbao kubwakubwa za mierezi ambazo ziliwekwa kwa ajili ya kulinda paa

Milango na miimo yake ilikuwa ya mraba

"fremu ngumu za umbo la mstatili"

1 Kings 7:6

Taarifa kwa ujumla

Mwandishi anaandika juu ya muundo wa ukumbi wa nguzo.

baraza

sehemu ya jengo ambayo imejengwa kwa safu ambayo inaunganisha sehemu zingine za jengo pamoja na lango.

1 Kings 7:7

Taarifa kwa ujumla

Mwandishi anaandika juu ya ukumbi wa ikulu

Sulemani akaijengabaraza yenye kiti cha enzi

"Sulemani alijenga nyumba iliyoitwa "nyumba ya kiti cha mfalme"

ilikuwa imeezekwa kwa mierezi

"wafanyakazi waliizeka ile nyumba kwa mierezi"

kutoka sakafu moja hadi nyingine

sakafu yote ilikuwa ya mierezi, kutoka ukuta mmoja hadi mwingine.

1 Kings 7:8

Taarifa kwa ujumla

Mwandishi anaendelea kuandika juu ya eneo la ikulu.

1 Kings 7:9

Taarifa kwa ujumla

Mwandishi anaandika juu ya mawe yaliyotumika kujengea hayo majengo

Majengo hayo yalipambwa kwa vitu vya thamani, mawe ya thamani

"Wafanyakazi waliyanakishi hayo majengo kwa mawe ya thamani na vitu vya thamani"

mawe ya thamani, yaliyochongwa na kukatwa kwa msimeno kufuata vipimo sahihi na kulainishwa

Wafanyakazi waliyapima mawe na kuyakata kwa usahihi na kuyalainisha"

Mawe ya namna hii ndiyo yaliyotumika

"wafanyakazi waliyatumia mawe hayo"

kuwanzia kwenye msingi hadi juu, pia na nje hadi kwenye baraza

Mwandishi anasisitiza kuwa wafanyakazi walitumia mawe ya thamani kwenye msingi na hata jengo lote kwa ujumla.

Msingi ulijengwa

"Wale wafanyakazi waliujenga msingi"

Dhiraa

Takribani sentimita 46

1 Kings 7:11

mihimili ya mierezi

Mhimili ni ubao mrefu unaojengwa kwa lengo la kushikilia kitu fulani kwenye mfumo wa ujenzi

safu tatu za mawe yaliyokatwa na safu moja ya mihimili ya mierezi

Tazama 6:36.

1 Kings 7:13

Kumleta Huramu kutoka Tiro

Huramu aliupokea wito wa Sulemani wa kuja Yerusalemu

mwana wa mjane ... baba yake alikuwa mtu wa Tiro

Mjane ni mwanamke ambaye mume wake alishafariki, na tunajiridhisha kuwa baba yake kweli alishakufa.

Huramau alikuwa mwingi wa hekima na ufahamu na stadi

Neno "hekima naufahamu" yanamaanisha kitu kilekile, yametumika kuonyesha msisitizo. "Mungu alimjaza Huramu kwa hekima, ufahamu na stadi"

1 Kings 7:15

Dhiraa kumi na nane

Dhiraa moja ni sentimita 46

mzingo wa mita 5.5

"mzingo" ni kipimo cha urefu wa kitu cha duara.

Akatengeneza taji mbili

Neno "taji" linamaanishapamba linalowekwa juu ya nguzo.

shaba

Shaba iling'aishwa ili kuaksi mwanga wa jua

Kulikuwa na nyavu za kuwa kama kaziy a kusuka

"Mikufu ya vyuma iliyosukwa"

1 Kings 7:18

safu mbili za komomanga

Komamanga ni tunda lenye ganda gumu, rangi nyekundu kwa ndani na mbegu nyingi zenye maji matamu. Huramu hakutumia makomamanga halisi kupamba hizo nguzo. Atengeneza kwa kutumia shaba.

Zile taji ...zilikuwa zimepambwa kwa maua, vyenye vimo vya mita 1.8

"Huramu alizipamba zile taji ... kwa maua ya shsaba, yenye vimo mita 1.8"

vichwa vya nguzo za ukumbi

Tazama 7:6

1 Kings 7:20

makomamanga mia mbili

"makomamanga 200"

Alisimamisha nguzo

Neno "Ali" linamaanisha wafanyakazi wa Huramu. "Wafanyakazi wa Huramu walisimamisha nguzo"

Ile nguzo ya kuume akaipa jina la Yakini

"jina la nguzo ya kuume illitwa Yakini"

Ile nguzo ya kushoto ilikuwa inaitwa Boaz

"Jna la nguzo ya kushoto iliitwa Boazi"

Hivyo ndivyo zile nguzo zilivyotengenezwa

"Hivyo ndivyo Huramu alivyozipamba zike nguzo"

1 Kings 7:23

bahari ya kusubu

Hi inamaanisha kalai la shaba ambalo liliweza kubeba maji.

vyuma vya kusubu

Huramu aliyeyusha shaba na kuvitengeneza

mita 2.3 kutoka ukingo hadi ukingo

kutoka ukingo mmoja hadi mwingine

mzingo wake ulikuwa mita 13.7

"mzingo" ni kipimo cha urefu wa mzunguko wa kitu cha dauara.

na vibuyu vilivyoizunguka

Kibuyu ni aina ya mboga yenye ganda gumu na lenye duara ambalo huoteshwa kwenye shamba la mizabibu.

wakati bahari inapokuwa kalibu

"wakati Huramu alipoitengeneza bahari"

1 Kings 7:25

Bahari

Bahari ya kutengeneza ya shaba

Bahari ilikaa juu ya

"ilikuwa juu ya"

Ile bahari iliwekwa juu yao

"Wafanyakazi wa Huramu walliweka bahari juu ya wale makiasai wa shaba

pande zao zote za nyuma

Hii ni sehemu ya nyuma ya mwili wa mnyama mwenye miguu minne

na ukingo wake ulikuwa kama ukingo wa kikombe, kama ua l a yungi

"Huramu aliitengeneza ukingo ukafanana n a ukingo wa kikombe, ukapinda kwa nje kama ua"

bathi elfu mbili

bathi moja ni sawa na lita 22.

1 Kings 7:27

urefu wa mita 1.8

Huo ni urefu wa kalio moja

Hivi ndivyo kazi za makalio zilivyofanywa

Hii inamaanisha kuwa mwandishi atayafafanua makalio katika maneno yafuatayo.

na juu ya papi na vipandio kulikuwa na simba, makisai, na makerubi

Kulikuwa na vipande vya nakshi katikasura za simba, makisai, na makerubi yaliyokuwa yameunganishwa katika pande za makalio.

masongo ya kazi y a kufuliwa

Neno "masongo" linamaanishsa vipande vya shaba vyenye sura ya kusokotwa.

1 Kings 7:30

magurudumu ya shaba na vipini, na pande zake nne

kulikuwa na pini moja kwa kila jozi yamagurudumu. "magurudumu manne napini mbili"

pande zake nne

"pande nne za kila kwa kila kalio"

Chini ya birika yalikuweko mataruma ya kusubu yenye masongo

"Huramu aliweka mataruma yenye vipande vya sura ya masongo"

na ile taji ilikuwa

Neno "taji" inamaanisha kipande cha mviringo kilichokuwa kimesimama wazi ili kibebe yale makalai.

na papi zake zilikuwa za maraba

Tazama 7:27

1 Kings 7:32

yalikuwa ndani ya makalio

neno "yao" linamaanha zile papi na neno "ndani" linamaanisha jinsi ile mikono ilivyokuwa ilivyokuwa imechomekwa kwenye zile papi.

Yale magurudumu yalikuwa kama ya gari.

"Huramu alitengeneza yale magrurdumu kuwa kama magurudumu madogo ya gari"

Mikono yake, na maduara, matindi yake, na vipande vya ndani

Neno "yake" limaanishsa yale magurudumu.

1 Kings 7:34

Kulikuwa na mataruma manne katika pande zake nne za makaliio

"Kulikuwa na mataruma katika kila upande wa kalio"

kina cha sentimita ishirini na tatu

sentimita ishirini na tatu ni sawa na "nusu ya dhiraa moja"

na juu ya makalio mashikio yake na papi zakae zikawa zimeshikanishwa

"Huramu alishikamanisha mashikio yake na papi na juu ya kila kalio"

1 Kings 7:36

nayo ilikuwa imezungukwa

Neno "nayo" linamaanisha Makerubi, simba, n a miti ya mitende.

ilikuwa imezungukwa na masongo

Neno "masongo" linamaanisha sura za kusukwa za vipande vya masongo.

Yote yalikuwa yametengenezwa kwa kufanana

"Huramu alitenegeneza makalio yote katika mfumo uleule"

na yalikuwa na vipimo sawa, na sura inayofanana

"makalio yote yalikuwa na vipimo sawa na sura sawa"

1 Kings 7:38

bathi arobaini

Bathi moja ni sawa na lita 22

upande wa mashariki, ukielekea upande wa kusini wa hekalu

"upande wa kusini mashariki wa hekalu"

1 Kings 7:40

lile besini la kuwa kama taji

mataji yalikuwa na sura kama ya beseni

mapambo ya kufunika

"mikufu ya vyuma iliyosukwa"

1 Kings 7:42

makomamanga mia nne

"makomamanga 400"

1 Kings 7:44

Akatengeneza

neno "aka" linamaanisha Hurama na wasaidizi wake.

na vyombo vingine vyote

"zana zingine zote"

shaba iliyosuguliwa

shaba inayong'aa na kuaksi mwanga

1 Kings 7:46

Mfalme alivisubu

"Mfalme alimruhusu Huramu awaagize wafanyakazi wake kuvisubu"

uwanda wa Yorodani

Hii inamaanisha eneo lililo tambarare karibu na Mto wa Yorodani.

kati ya Sukoti na Zarethani

"Sukoti" ni mji ulio upande wa mashariki mwa Mto Yorodani

Sulemani hakuvipima vyombo vyote

"Sulemani hakumwambia Huramu na wafanyakazi wake kuvipima vyombo vyote"

kwa sababu uzani wa shaba ulikuwa hauwezi kupimwa

"hakuna ambaye angeweza kuupima uzani wa shaba"

1 Kings 7:48

Sulemani akatengeneza

"Wafnyakazi wa Sulemani walitengeneza"

ile meza ambayo iliwekwa mikate ya wonyesho

"ambayo makuhani waliweka mikate ya wonyesho"

maua, na taa

"maua" na "taa" vilikuwa sehemu ya vinara.

1 Kings 7:50

Vile vikombe ... vilikuwa vimetengenezwa kwa dhahabu

"Wafanyakazi walivitengeneza vikombe ... kwa kutumia dhahabu halisi"

Na bawaba ... vyote vilitengenezwa kwa dhahabu

"Pia walizitengeneza bawaba ... kwa kutumia dhahabu"

bawaba za milngo

bawaba in aweza kumaanisha ima 1)bawaba ambazo huruhusu milango kugeuka, au 2) mashikio mabayo hushikilia milango.

1 Kings 7:51

kazi yote ambayo mfalme Sulemani kwa ajili ya hekalu ilimalika

wafanyakazi waliimaliz kaziyote ambayo Sulemani aliwataka wafanye kwa ajili ya nyumba ya BWANA"

1 Kings 8

1 Kings 8:1

akawakusanya wazee wa Israeli

"aliwaita pamoja viongozi wa Israeli"

wanaume wote

Hii yaweza kumaanisha 1) watu ambao Sulemani aliwaita kule Yerusalemu ambao pia wameorodheshwa kwenye 8:1 au 2) kwa wale ambao walisafiri kwenda Yerusalemu kwa ajili ya sikukuu, na siyo lazima kuwa ni wanaume wote walioishi Israeli.

Kwenye sikukuu

Hii inamaanisha sikukuu ya vibanda

Katika mwezi wa Ethanimu, ambao ndio mwezi wa saba

"Ethanimu" ni m Huu mwezi ulikuwa kati ya mwezi wa saba wa kalenda ya Kihebrania. Huu mwezi ulikuwa kati ya sehemu ya mwisho wa mwezi wa Septemba na mwanzoni mwa mwezi wa Oktoba kwa kalenda ya Magharibi.

1 Kings 8:3

ambazo hazikuweza kuhesabiwa

"ambazo hakuna mtu aliyekuwa na uwezo wa kuzihesabu"

1 Kings 8:6

ndani ya chumba cha ndani, mahali patakatifu sana

Sentensi ya pili inatumika kufafanua sentensi ya kwanza.

miti yake kwani ilitumika kulibebea

"miti ambayo makuhani walitumia kulibebea"

haikuweza kuonekana

"hakuna aliyeweza kuwaona"

1 Kings 8:9

ilitokea kwamba

Kirai hiki kimetumika hapa ili kuonyesha tukio la muhimu katika habari. Kama lugha yako ina namna ya kuonyesha hilo, unaweza kuitumia

1 Kings 8:12

makao ya kujivunia

"Nyumba iliyoinuliwa"

1 Kings 8:14

BWANA, Mungu wa Israeli, asifiwe

"Msifuni BWANA, Mungu wa Israeli"

kwa mkono wake

"kwa nguvu zake"

1 Kings 8:17

ilikuwa kwenye moyo wa Daudi

"ilikuwa hamu ya Daudi"

mmoja wa wanao atakayezaliwa toka viunoni mwako

"mmoja mabye atakuwa mzaliwa wa wana wako" au "mmoja ambaye wewe utakuwa baba kwake"

1 Kings 8:20

nimeketi kwenye kiti cha enzi cha Israeli

"Ninatawala juu ya Israeli"

1 Kings 8:22

hutembea mbele yako kwa mioyo yao yote

"kuishi kwa moyo wote ambao wewe unapenda waishi"

umetimiza kwa mkono wako

"kwa nguvu zako umetimiza ulichosema"

1 Kings 8:25

ataketi katika kiti cha enzi cha Israeli

"kuitawala Israeli"

kutembea mbele yangu

"kuishi kwa kunitii mimi"

1 Kings 8:27

Je, ni kweli Mungu ataishi duniani?

"Lakiini kwa hakika haiwezekani kuwa Mungu ataishi duniani!"

maombi haya ya mtumishi wako na haja yake

Neno "maombi" na "haja" yanamaanisha kitu kilekile. Yametumika kuonesha msisitizo wa maombi yake.

uyajali maombi haya ya mtumishi wako ... sikiliza kilio na maombi ambayo mtumishi wako anakuomba leo

sehemu ya kwanza na ya mwisho ya sentensi hizi zinamaanisha kitu kilekile. Sehemu zote zinaonesha maombi ya Sulemani.

1 Kings 8:29

Naomba ulitazame hekealu hili

"Naomba uliangalie"

mchana nausiku

"wakati wote" au "kila mara"

Jina langu na uwepo wangu

Maneno haya kwa pamoja yanasisitiza kuwa BWANA ataishi hekaluni.

1 Kings 8:31

anapewa sharti la kiapo

mtu mmoja anamtaka aape

kichwani mwake

kichwa kinamaanisha mtu kamili. "juu yake"

thawabu yake ya haki

"kile anachohitaji kwa sababu ya kutokuwa na hatia"

1 Kings 8:33

Watu wako Israeli watakapopigwa na adui

adui amewashinda watu wako Israeli

1 Kings 8:35

mbingu zitafungwa na mvua hazinyeshi

Virai vyote viwili vinamaanisha kitu kilekile

njia njema itakayowapasa

"ambayo kwayo wanatakiwa kuishi"

1 Kings 8:37

magonjwa au ukungu

haya nimajina ya magonjwa ya mazao ya kilimo yanayomaanisha kifo cha mazao kutokana uhaba wa mvua au mvua iliyozidi.

nzige au funza

"nzige" niaainaya panzi ambaye husababisha uharibifu kwa njia ya kula mazao, Neno "funza" ni hatua ya mwanzo wa kukua kwa nzige.

na kama kuna mtu au watu wataomba

mtu au watu wako wote wa Israeli, wataomba na kukupa dua"

akaijua hiyo tauni katika moyo wake

Hii inaweza kumaanisha 1) "kuijua dhambi katika moyo wake" au 2) "kujua katika moyo wake kwamba ile tauni ni matokeo ya dhambi yake

1 Kings 8:39

mbinguni, angani

mbinguni ni mahali ambapo Mungu huishi. Pia linaweza kumaanisha angani kutemea na mukhutadha. Lakini mbinguni ni mahali pa juu ya ardhi au dunia.

uhai, kuishi, maisha, aliye hai

maneno haya yote yanamaanisha kuwa hai kimwili.

samehe, msamaha

kumsamehe mtu kunamaanisha kutokushikilia hasira dhidiya mtu aliyekuumiza.

zawadi

zawadi linamaanisha kitu ambacho mtu hupokea kwa sababu ya kufanya kitu fulani

moyo

katika biblia, neno "moyo" limetumika kama lugha ya umbo kumaanisha mawazo, hisia, tamaa au utashi.

hofu, kuogopa, hofu ya BWANA

Nno "hofu" na "kuogopa" yanamaanisha hisisa hasi ambazo mtu huwa nazo pale kunapokuwepo na kitisho. Lakini pia neno "hofu" linamaanisha heshima ya ndani kabisa kwa mtu mwenye mamlaka.

1 Kings 8:41

mkono wako wenye nguvu, na mkono wako ulioinuliwa

Virai hivi viwili vinamaanisha kitu kilekile na vivnalenga mamlaka ya Mungu.

nyumba hii niliyoijenga inaitwa kwa jina lako

Kirai kinachosema "inaitwa kwa jin lako" kinamaanisha umiliki. "wewe ndiye mmiliki wa nyumba hii ambayo nimeijenga"

1 Kings 8:44

maombi yao, na dua zao

Neno "maombi" na "dua" yana maana moja yametumika kuonyesha juhudi ya kile ambacho watu wanamwomba BWANA awafanyie.

1 Kings 8:46

kutokea katika nchi ya watekaji

"ambako adui zao wamewapeleka kama mateka"

katika nchi ya watekaji

Neno "watekaji" linamaasha wale watu ambao huwafanya watu kuwa mateka.

Tuemetenda kwa ukaidi, na tumefanya dhambi. Tumetenda kwa uovu.

Virai hivi viwili vinvamaanisha kitu kimoja na vimetumika kuonyesha msisitizo wa jinsi hawa watu walivyofanya mabaya.

tumetenda kwa ukaidi, na tumefanya dhambi

Maneno haya mawili ya namaanisha kitu kilekile na yametumika kuonyesha jinsi wale watu walivyofanya uovu.

1 Kings 8:48

kwa mioyo yao yote na kwa roho zao zote

Tazama 2:1

kuelekea nchi yao

Neno "nchi yao" linamaanisha nchi ya walke wanaoomba, nayo ni, Israeli.

1 Kings 8:49

maombi yao, dua zao

Tazama 8:44

Wasamehe watu wako waliotenda dhambi dhidi yako, na dhambi zao zote ambazo kwazo, wamekukosea wewe dhidi ya amri zako

Sulemani anamwomba BWANA mara mbili kuwasamehe watu. Hii inasisitiza ile juhudi ya dua yake.

1 Kings 8:51

tanuru ambamo vyuma huyeyushwa

"tanuru ambalo watuhuyeyusha vyuma"

macho yako yatazame

"utazingatia"

1 Kings 8:54

Asiwe BWANA

"Msifuni BWANA"

1 Kings 8:57

Asituache wala kututelekeza

Virai hivi viwili vinamaanisha kitu kilekile na vinasisitza hamu ya BWANA ya kuwa pamoja na watu.

aunganishe mioyo yetu na yeye

"atufanye tujitoe kwake"

tuishi katika njia zake

"kuishi kama anavyotutaka kufanya"

1 Kings 8:59

mchana na usiku

"muda wote"

mioyo yenu iwe ya haki

"kujitoa kikamilifu"

1 Kings 8:62

watu pamoja naye

Tazama 8:1

1 Kings 8:64

madhabahu ya shaba iliyokuwa mbele yakae

"madhabahu ya shaba iliykuwa mbele ya BWANA"

1 Kings 8:65

Israeli yote pamoja naye

Tazama 8:62

siku saba ... siku saba ... siku kumi na nne

"siku 7 ... siku 7 ... siku 14"

kwa furaha na mioyo ya shangwe

Virai hivi viwili vinmaanisha kitu sawa

1 Kings 9

1 Kings 9:1

Sulemani

Sulemani alikuwa mwana wa mfalme Daudi ambaye alikuwa mtoto wa Bthisheba.

nyumba

neno nyumba limetumika kama lugha ya umbo katika biblia. Wakati mwingine limemaanisha "wanafamilia", wakati mwingine limemaanisha uzao wa mtu fulani, na wakati mwingine limemaanisha Hekalu au masikani ya BWANA. Pengine limemaanisha watu wa Mungu na wakati mwingine taifa la Israeli.

BWANA

Neno "BWANA" ni jina binafsi la Mungu ambalo lilijifunua wakati wa Mungu alipojidhihirisha kwa Musa kwenye kile kichaka kilichokuwa kinawaka moto.

mfalme

Neno "mfalme" linamaanisha mtu mwenye mamlaka makubwa ya mji, serikali au ya nchi.

Ikulu

Neno "ikulu" linamaanisha nyumba anayoishi mfalme, pamoja n a wanafamilia wake, na watumishi wake.

Gibioni, Wagibioni

Gibioni ni mji uliokuwa umbali wa kilomita 13 kaskazini m ashariki mwa Yerusalemu. Watu waliokuwa wakiishi kwenye huo mji waliitwa Wagibioni.

1 Kings 9:3

ili niweke jina langu humo milele

"ili kuishi humo na kuwa mmliki milele na milele"

Macho yangu na moyo wangu utakuwa humo nyakati zote

"Nitalilinda na kulitunza"

1 Kings 9:4

kama utatembea mbele yangu kama baba yako Daudi alivyotembea

"Kama utaisha kama ninavyokutaka uishi, kama vile Daudi baba yako alivyofanya"

kwa haki na unyofu katika moyo

Virai hivi viwili vinamaanisha kitu kilekile, vimetumika kuonyesha msisitizo wa jinsi Daudi alivyokuwa.

kiti chako cha enzi

"utawala wako"

uzao wako hautaondoka katika kiti cha enzi cha Israeli

"daima utatawala katika Israeli"

1 Kings 9:6

amri zangu na maagizo yangu

"maagizo" na "amri" yanamaanishakitu kilekile yametumika kusisitiza kuwa BWANA aliamuru.

kuabudu miungu mingine na kusujudu

Virai hivi vinamaanisha kitu kilekile, na vimeunganiswa kwa ajili ya msisitizo.

niliyoitakasa kwa jina langu

"niliyoitenga kwa ajili yangu"

Nitaitupilia mbali

"Nitaikataa"

1 Kings 9:8

Ijapokuwa hekalu hili limetukuka sasa

"japokuwa hekalu hili ni kubwa na zuri"

atasituka na kuzomea

"ataonyesha mshangao na kutoa sauti ya dharau"

wameinamia na kuiabudu

Virai hivi vinamaanisha kitu kilekile. Kirai "kuiinamia" kinaonyesha kitendo ambacho watu hutumia wa wakati wa kuabudu.

1 Kings 9:10

Ilitokea

Nneo hili limetumika ili kuonesha mwanzo mpya wa habari. Unaweza kutumia neneo ambalo lugha yako huwa inatumia.

mwishoni mwa miaka ishirini

"baada ya miaka 20"

Sulemani alikuwa amemaliza kuyajenga

"Wafanyakazi wa Sulemani walikua wamemaliza kuyajenga"

1 Kings 9:12

Ndugu yangu, ni miji gani hii uliyonipa?

"Hii miji uliyonipa ni mizuri lakini haina faida yeyote."

akaiita nchi ya Kabuli mpaka leo

"Na watu bado huiita hivyo mpaka leo"

tani alfu nne za dhahabu

"kiasi cha kilogramu 4000"

1 Kings 9:15

vigezo ambavyo Sulemani aliweka ili kujenga hekalu

"sababu ambazo Sulemani aliweka kwa wafanyazi ili wajenge hekalu"

kuijenga Milo

Inaweza kumaanisha "kujenga ule mfumo wa ngazi"

Farao mfalme wa Misiri alikuwa ameenda

"Jeshi la Farao, mfalme wa Misri, lilikuwa limeenda"

1 Kings 9:17

Kwa hiyo Sulemani akaijenga Gezeri

"Wafanyakazi wa Sulemani wakaijenga Gezeri"

1 Kings 9:20

makundi ya watu, watu wengi, watu, mtu

Hayao ni , makundi ya watu wenye lugha moja na utamaduni mmoja.

Mwamori

Waamori walikuwa watu wenye nguvu ambao walikuwa wanatokana na mjukuu wa Nuhu aliyeitwa Kanaani.

Mhiti

Wahiti walitokana na uzao wa Hamu kupitia mwanae Kanaani. Baadaye walikuja kuwa dola kubwa ambayo leo iko kwenye eneo la Uturuki na Palestina y a kaskazini.

Waperezi

Waperezi walikuwa moja ya makundi ta watu waliokuwa katika nchi ya Kanaani. Tunafahamu machache sana juu ya mababu wa hili kundi na hata sehemu hasa walikoishi huko Kanaani

uzao, walitokana n a

"uzad" ni mtu ambaye ana uhusiano wa moja kwa moja au uhusiano wa damu na mtu katika historia.

Yebuse, Wayebuse

Wayebuse walikuwa ni moja ya makundi ya watu walioishi katika nchi ya Kanaani. Walitokana na mtoto wa Hamu aliyeitwa Kanaani.

kazi, wafanya kazi

Neno "kazi" linamaanisha kufanya kazi fulani ngumu.

1 Kings 9:22

Sulemai hakuwafanya kuwa shokoa watu wa Israeli

"Sileani hakuwashurutisha watu wa Israeli kufanya kazi"

1 Kings 9:23

watu 550

"watu mia tano na hamsini"

1 Kings 9:24

akaijenga Milo

Tazama 9:15

1 Kings 9:25

madhabahu iliyokuwa mbele ya BWANA

Tazama 8:64

Kwa hiyo akalimaliza hekalu

"Kwa hiyo wafanya kazi wake wakalimaliza hekalu"

1 Kings 9:26

Sulemani alitengeneza

"Wafanyakazi wa Sulemani walijenga"

Merikebu

"kundi kubwa la meli"

tani 14.5 za dhahabu

"kiasi cha kilo 14,000 za dhahabu

1 Kings 10

1 Kings 10:1

Uvumi wa Sulemani kuhusu jina la BWANA

Inaweza kumaanisha 1) "Uvumi wa Sulemani uliomtukuza BWANA" au 2) "Uvumi wa Sulemani aliopewa na BWANA"

yote yaliyokuwa moyoni mwake

"vyote alivyotaka kujua"

1 Kings 10:3

kuketi kwa watumishi wake

Inaweza kumaanisha 1) "Jinsi watumishi wake walivyokuwa wameketi kuzunguka meza" au 2) "Mahli ambapo watumishi wake waliishi"

roho yake ilizimika

"aliishiwa pumzi"

1 Kings 10:6

maneno yako na hekiima yako

Neno "hekima" linbeba uzito wa "maneno". "hekima ya semi zako"

macho yangu yamejionea

"Nimejionea"

Hata nusu ya hekima na utajri wako umezidi uvumi ambao nilikuwa nimesikia

"watu waliniambia kidogo sana"

1 Kings 10:8

ambao daima husimama mbele yako

"ambao wako katika uwepo wako wakisubiri kukutumikia"

BWANA, Mungu wako atukuzwe

"Watu na wamtukuze BWANA Mungu wako"

alikuweka kwenye kiti cha enzi cha Israeli

"Aliyekufanya kuwa mfalme"

1 Kings 10:10

kilo za dhahabu elfu nne na miatano

kilo 4500 za dhahabu

Hapakuwahi kutokea kiasi kikubwa cha viungo ... alitoa kwa mfalme Sulemani kuwahi kutolewa tena

"Hakuna tena mtu aliyetoa kwa mfalme Sulemani viungo kama vile ambavyo malkia wa Sheba alimpa"

1 Kings 10:11

Mfalme alitengeneza nguzo

"Wafanyakazi wa mfalme walitengeneza nguzo za hekalu"

kimewahi kutokea hadi leo

"wala hakuna aliyewahi kuona kiasi kikubwa tena"

1 Kings 10:13

kila kitu ambacho alihitaji, na kila kitu alichoomba

Virai hivi viwili vinamaanisha kitu kilekile na vitumika kwa pamoja kuonyesha msisitizo.

kwa ukarimu wake

"kutokana na ukarimu wake"

1 Kings 10:14

kwa mwaka mmoja

Hii inamaanisha kwa kila mwaka katika utawala wa Sulemani, na wala siyo mara moja tu. "kila mwaka"

kilo elfu ishrini na tatu za dhahabu

kilo 23,000za dhahabu

1 Kings 10:16

Mfalme Sulemani alitengeneza

"wafanyakazi wa mfalme Sulemani walitengeneza"

ngao kubwa mia mbili

"ngao 200 kubwa"

shekeli mia sita za dhahabu

Shekeli moja ina kipimmo ch a gramu 11. "Ni kama kiasi cha kilo 6.6 cha dhahabu"

shekeli mia sita

ni sawa na kilo tatu

ngao mia tatu

"ngao 300"

Mane tatu za dhahabu

Mane moja ni kipimo kilicho karibu sawa na gramu 600."sawa na kiasi cha kilo 1.8 za dhahabu"

ikulu ya mwitu wa Lebanoni

Tazama 7:1

1 Kings 10:18

mfalme akafanya

"wafanyakazi wa mfalme walifanya"

enzi kwa pembe

Pembe ni vitu vigumu vyeupe ambavyo vinatokana na pembe za tembo.

1 Kings 10:21

ikulu ya mwitu wa Lebanoni

Tazama 7:1

1 Kings 10:23

wote ulimwenguni

"watu kutoka sehemu zote"

ilitafuta uwepo wa Sulemani

"walitafuta kumtembelea Sulemani"

ambayo Mungu alikuwa ameweka katika moyo wake

"ambacho Mungu alikuwa ameweka katika akili zake" au "ambacho Mungu alikuwa amempatia"

1 Kings 10:26

magari 1,400 na wapanda farasi elfu kumi na mbili

"magari 1,400 na wapanda farasi 12,000"

1 Kings 10:28

waliokuwa wamenunuliwa kutoka Misri

"amabao wachuuzi wake waliwanunua Misri"

Magari yalinunuliwa

"Wachuuzi wake walinunua magari"

kwa shekeli mia sita za fedha ... shekeli 150

Shekeli moja ina uzani wa ulioswa na gramu 11. "karibu sawa na kilo 6.6 za fedha ... sawa na kilo 1.7"

Vitu vingi katika hivi baadaye viliuzwa

"Wachuuzi wake baadaye waliviuza vitu hivi"

1 Kings 11

1 Kings 11:1

Wamoabu, Waamori, Waedomu, Wasidoni na Wahiti

Haya ni majina ya makundi ya watu

Basi mfalme Sulemani

Neno "basi" linaonyesha mwanzo wa habari mpya.

wataigeuza mioyo yenu ili mfuate miungu yao

"watawashawishi kuabudu miungu wanayoiabudu"

1 Kings 11:3

wanawake halali mia saba namasuria mia tatu

"wanawake halali 700 na masuria 300"

waliugeuza moyo wake

"waliugeuza moyo wake toka kwa BWANA" au "walimgeuza akaacha kumwabudu BWANA"

hakuutoa moyo wake wote

"hakuwa amejito akikamilifu"

1 Kings 11:5

Ashitorethi, Milikomu

Haya ni majina ya miiungu ya uongo

Wasidoni

Hili jinala kundi la watu

maovu mbele ya BWANA

"kile ambacho BWANA alikiona kuwa ni kiovu"

alimfuata Milikomu

"Milikomu" ni jina lingine la "Moleki"

1 Kings 11:7

walifukiza uvumba na kuwatolea sadaka

Neno "kuwa" linamaanisha hao miungu ambao Sulemani aliwajengea.

1 Kings 11:9

Moyo wake ulikuwa umemwacha Mungu

"Sulemani alimwacha kumwabudu BWANA"

alikuwa amejionyesha kwake mara mbili

"BWANA alikuwa amejionyesha kwa Sukemani mara mbili"

1 Kings 11:11

nitaugawa ufalme kutoka kwako

Mungu atauondo ufalme kutoka kwenye uzao wa Sulemani kama vile mtu achanavyo kipande cha nguo.

ukiwa chini ya mwanao

"mamlaka ya mwanao"

1 Kings 11:14

Daudi alipokuwa Edomu ... Hadadi alipokuwa mtoto mdogo

Hii ni habari ya historia iliyotokea hapo kale.

Yoabu na Israeli yote

"Yoabu na jeshi lote la Israeli"

Hadadi alichukuliwa na Waedumu wengine na watumishi wa baba yake

"watumishi wa baba wa Hadadi walimchukua pamoja na Waedomu wengine"

1 Kings 11:18

Taarifa kwa ujumla

Tazama 4:11

Waliondoka Midiani

Tazama 11:14

1 Kings 11:20

Daudi alishalala na mababu zake

"Daudi alikuwa amekufa"

1 Kings 11:23

Daudi aliwapiga

Wakati jeshi la Daudi lilkipowaua

Rezoni akawachukia Israeli

"Rezoni aliwachukia sana Waisraeli"

1 Kings 11:26

akainua mkono wake dhidi ya mfalme

"akamwasi mfalme"

Sulemani kujenga Milo

Tazama9:15

1 Kings 11:28

Mtu hodari na shujaa

Inaweza kumaanisha 1) "shuja mkuu" 2) "mtu mwenye uwezo mkubwa" au 3)mtu tajiri na mwenye ushawishi."

akampa kuwa na mamlaka

"akamfanya kuwa kamanda"

1 Kings 11:31

Akamwabia

Neno "a" linamaanisha Ahiya

Nitaugawa ufalme

Tazama 11:11

mkono wa Sulemani

"mamalaka ya Sulemani

Sulemani atabaki

"Mwana wa Sulemani a" au "Uzao wa Sulemani utabaki"

kilicho chema katika macho yangu

"Ninachokiona kuwa sawa"

1 Kings 11:34

Taarifa kwa ujumla

Ahiya anaendelea kumwambia Yeroboamu kile ambacho BWANA alisema.

Sitauchukua

"Neno "si" linamaanisha BWANA

kwenye mkono wa Sulemani

"toka kwenye mamlaka ya Sulemani"

Nitampa

Neno "m" Yeroboamu.

atabaki kuwa nuru mbele yangu

"daima kutakuwa na kizazi kitakachotawala ili kuwa ukumbusho wa familia ya Daudi"

1 Kings 11:37

Taarifa kwa ujumla

Ahiya anaendeleea kumwambia Yeroboamu kile ambacho BWANA amesema.

Nitakuchukua

Neno "ni" linamaanisha BWANA na neno "ku" linamaanisha Yeroboaomu.

kinachopendeza mbele yangu

Tazama 1:31

nitakujengea nyumba ya uhakika

"Nitakuanzia ufalme wa milele"

1 Kings 11:40

Yeroboamu

Yeroboamu mwana wa Nebati ndiye aliyekuwa mfalme wa kwanza wa dola ya kaskazini ya Israeli kati ya mwaka 910 - 900 KK. Yeroboamu mwingine, mwana wa Yehoashi, alitawala Israeli baada ya miaka 120

Misri, Wamisri

Misri ni nchi iliyo kasikazini mwa Afrika, kusini magharibi mwa nchi ya Kanaani.

kifo. kufa, aliyekufa

Neno hili linatumika kuonyesha kifo cha kimwili na cha kiroho.

1 Kings 11:41

je, hayakuandikwa katika kitabu cha matukio y a Sulemani?

"unaweza kuyapata kwenye kitabu cha matukio ya Sulemani."

Kitabu cha matukio ya Sulemani

hiki ni kitabu ambacho kwa sasa hakipo tena

Naye akalala na mababu zake

"Akafa"

alizikwa

"watu wakamzika"

1 Kings 12

1 Kings 12:1

Israeli yote walikua wanaenda

"Wanaume wote wa Israeli"

Ikatokea kuwa

Neno hili linaonyesha mwanzo wa habari mpya. Waweza kutumia neno lililo katika lugha yako.

1 Kings 12:3

kumwita

Herufi "m" inamaanisha Yeroboamu

ailiifanya nira yetu kuwa nzito

"alitutendea kwa ukatili" au "alitushurutisha kufanya kazi"

1 Kings 12:6

kwa wazee waliokuwa wamesimama mbele ya Sulemain

"wazee waliomshauri Sulemani" au "wazee waliohudhuria kwa Sulemani"

1 Kings 12:8

wakasimama mbele yake

"waliomshauri" au "waliohudhuria kwake"

ifanye nyepesi nira ambayo baba yako alituwekea"

"usitutenee kwa ukatilii kama baba yako alivyotutendea" au "usitushurutishe kufanya kazi kama baba yako alivyotufanyia"

1 Kings 12:10

kidole changu kidogo ni kinene kuliko kiuno cha baba yangu

Maana yake ni kwamba Rehoboamu ni mkali na mwenye kuogofya kuliko baba yake.

Baba yangu aliwaadhibu kwa mijeredi, lakini mimi nitawaadhibu kwa nge

Hii inamaanisha kuwa adhabu ambayo Rehoboamu ataitoa ni mbaya kuliko alitoa baba yake.

nitawaadhibu kwa nge

Neno "nge" linaweza kumaanisha 1)mjeredi wenye ncha za vyuma, au 2) kiumbe mwenye mkia wa sumu.

1 Kings 12:12

baba yangu aliwatwika kongwa zito ... mimi nitawaadhibu kwa nge

Tazama 12:10

1 Kings 12:15

kwa kuwa ilikuwa zamu ya tukio lililoletwa na BWANA

"BWANA alisababisha hili litokee"

1 Kings 12:16

Israeli yote

"watu wote wa Israeli waliokuwepo"

Je, tuna sehemu gani kwa Daudi?

"hatutakuwa na sehemu katika familia ya Daudi"

Hatuna urithi kwa mwana wa Yese"

"Hatutakuwa na chochote cha kufanya katika uzao wa Yese"

"Nenda kwenye hema zako

"Nendeni nyumbani kwenu, enyi watu wa Israeli"

sasa tazama kwenye nyumba yako

"Sasa uuangalie utawala wako, uzao wa Daudi"

1 Kings 12:18

Waisraeli wote wakampiga kwa mawe

"Watu wote wa Israeli waliokuwepo pale"

nyumba ya Daudi

"Wafalme wanaotokana na uzao wa Daudi"

1 Kings 12:20

Ndipo Israeli

Neno hili limetumika kuonesha kuwa kuna tukio la muhimu kwenye habari. Waweza kutumia neno lolote lililo kwenye kabila yako lenye mukhutadha huo.

Israeli yote

"Viongozi wote wa Israeli waliposikia"

kuwa mfalme wa Israeli

"mfalme wa makabila yote 10 ya Israeli"

familia ya Daudi

"Uzao wa Daudi"

kabila ya Yuda

"watu wa kabila ya Yuda"

1 Kings 12:21

nyumba ya Yuda

Watu kutoka kabil ya Yuda

wanaume wanajeshi 180,000

"askari 180,000 waliochaaguliwa kwa uangalifu" au "askari wazuri 180,000"

nyumba ya Israeli

watu kutoka makabila 10 ya Israeli yaliyokuwa kaskazini

1 Kings 12:22

Neno la Mungu lkamjia

"Mungu alisema neno lake"

mtu wa Mungu

Hili jina lingine la nabii, "Nabii"

kwa nyumba yote ya Yuda na Benjamini

"watu wote wa kabila Yuda na Benjamini"

ndugu zako watu wa Israeli

Neno "ndugu" na "watu wa Israeli" vyote vivnamaanisha wanaume wa makabila kumi ya kaskazini mwa Israeli na vinatoa msisitizo wa uhusiano wa kifamilia kati yao na Rehoboamu.

kwa kuwa jambo hili nimelisababisha mimi

"Kwa sababu mimi ndiye niliyelifanya litokee"

1 Kings 12:25

Yeroboamu akaijenga Shekemu

"Wafanyakazi wa Yeroboamu wakaijenga Shekemu"

akafikiri moyoni mwake

"mwenyewe akafikiri"

nyumba ya Daudi

"wafalme waliotokana na Daudi"

Kama hawa watu wataenda

Neno "watu hawa" linamaanisha wale watu wa makabila kumi ya Waisraeli wa kaskazini.

basi mioyo ya hawa watu itarudi tena kwa bwana wao, kwa Rehoboamu mfalme wa Yuda ... na kurudi kwa Rehoboamu mfalme wa Yuda

Virai hivi vina maana moja ambavyo vimetumika pamoja kuonesha msisitizo.

1 Kings 12:28

iliyowatoa toka

"iliyowatoa mababu zenu toka"

1 Kings 12:31

Yeroboamu akajenga nyumba mahali pa juu

"Wafanyakazi wa Yeroboamu walijenga nyumba mahali pa juu"

kufanya makuhani

"aliwachagua watu kuwa makuhani"

watu wote

"watu wote wa makabila kumi ya kaskazini"

katika mweziwa , wa siku ya kumi na tano ya mwezi

Huu ni mwezi wa nane wa kalenda ya Wahebrania. Siku ya kumi na tano ni kaaribu na mwanzo wa mwezi wa Novemba wa kalenda ya kimagharibi. "siku ya kumi na tano ya mwezi wa nane"

akaenda juu kwenye madhabahu

"akatoa sadaka kwenye madhabahu"

1 Kings 12:33

akaenda juu kwenye madhabahu

"akatoa sadaka madhabahuni"

ndio mwezialiokuwa amefikiri katika akili yake

"katika mwezi aliokuwa ameamua"

1 Kings 13

1 Kings 13:1

mtu wa Mungu

Hili jina lingine la nabii. "Nabii"

Alia kinyumem na zile madhabahu

"Alitoa unabii kwa sauti kubwa kinyume na zile madhdabahu"

Ee madhabau, madhabau

Nabii iliziambia zile madhabahu kama vile anamwambia mtu anyeweza kumsikia. Alisema mara mbili ili kusisitiza.

mwana aitwaye Yosia atazaliwa katikafamilia ya Daudi

"mwana wa uzao wa Daudi atakuwa na mwana aitwaye Yosia"

watachoma

Neno "wa" linamaanisha Yosia na watu atakaokuwa nao.

madhabahu zitavunjika, na majivu ylyo juu yatamwagika

"BWANA atazivunja madhabahu na atayasambaza majivu yaliyo juu yake"

1 Kings 13:4

Na ile madhabahu ikavunjika vipande vipande, na majivu yakamwagika kutoka madhabahuni

"Mungu akazivunja zile madhabahu na akayamwaga yale majivu kutoka madhabahuni"

kama iloivyokuwa imefafanuliwa kuwa ndiyo ishara ya kwamba mtu wa Mungu alikuwa amepewa kwa neno la Mungu

"kama ishara ambayo mtu wa Mungu alikuwa amefafanua kwa neno la BWANA"

1 Kings 13:6

mkono wangu urejee

" BWANA arejeshe mkoo wangu"

mkonio wa mfalme ukarejea

"BWANA alirejesha mkono wa mfalme"

1 Kings 13:8

Hata kama utanipa nusu ya milki yako. Sitaenda na wewe

"Unadhani kuwa kama utanipa nusu ya miliki yako nitaenda na wewe. Lakini hata kama utafanya hivyo, sitaenda na wewe"

1 Kings 13:11

Wale wanawe walikuwa wamemwona yule mtu Mungu kutoka Yuda njia aliyotumia

"wanawe walimwonyesha njia"

1 Kings 13:14

Yulenabii mzee

"Nabii kutoka Betheli"

akamwambia

"nabii mzee akamwambia mtu wa Mungu"

Naye akamjibu

"Mtu wa Mungu akamjibu"

mahali hapa

"Hapa Betheli"

1 Kings 13:18

malaika amesema nami neno la BWANA

"malaika ameniambia kile ammbacho BWANA amesema" au "malaika ameniambia ujumbe kutoka kwa BWANA"

1 Kings 13:20

Walipokuwa wamekaa mezani

"Walipokuwa wameketi mezani wakila"

Neno la BWANA likamjia yule nabii

Tazama 6:11

aliyemrudisha

Herufi "m" inamaanisha mtu wa Mungu

1 Kings 13:23

na mwili wake uliachwa barabarani

"na akaucha mwili wake barabarani"

walikuja wakaeleza

"walikuja wakawambia watu juu ya ule mwili"

1 Kings 13:26

neno la Mungu, neno la BWANA, neno la Bwana, maandiko

Katika biblia, "neno la Mungu" linamaanisha kitu chochite ambacho Mungu amesema kwa watu. Hii inajumuisha kilichoandikwa na kilichosemwa. Yesu pia anaitwa "neno la Mungu"

mwana, mwana wa

Neno "mwana" linamlenga mtoto wa kiume au mwanamume katiak uhusiano na mzazi wake. Inaweza pia kumaanisha mtoto wa kiume aliyeasiliwa.

1 Kings 13:29

wakamwombolezea

Hapa herufi "wa" inamaanisha yule nabii na wanawe.

Aa, ndugu yangu

Neno "Aa" linaonyesha huzuni kubwa

1 Kings 13:31

baada ya kumzika

alieyemzika ni yule nabii mzee, na herufi "m" inamaanisha yule mtu wa Mungu.

1 Kings 13:33

Jambo hiloi likawa dhambi kwenye familia ya Yeroboamu

"Familia ya Yeroboamu ikawa imefanya dhambi kwa kufanya jambo hili"

Jambo hili

Hii inamaanisha kitendo cha Yeroboamu kujenga madhabahu ya miungu na kuchagua makuhani.

na kusababishsa familia yake kuangamizwa na kuondolewa kabisa katika uso wa dunia

"Munugu aliiangamiza na kuiondoa familia ya Yeroboamu katika usowa dunia"

1 Kings 14

1 Kings 14:1

ili wasikutambue

"hakuna atakayekutambua"

1 Kings 14:4

Tazama, mke wa Yeroboamu

Neno "Tazama" linamaanisha "sikiliza kwa uangalifu"

Mwambie hivi na hivi

Neno "hivi" na "hivi" linamaanisha kuwa BWANA alikuwa amemwambia Ahiya kitu cha kusema. "mwabia hivi"

1 Kings 14:6

kwa nini unajifanya kuwa mtu mwingine?

Acha kujifanya kuwa mtu mwingine;Mimki najua kuwa wewe ni nani?

Nimetumwa kwako nikiwa na habari mbaya

"BWANA ameniambia nikwambie habari mbaya"

Niliugawa ufalme

Mungu aliugawa ufalme kama vile mtu achanavyo kipande cha nguo.

1 Kings 14:9

kunitupa nyumavyako

Yeroboamu ameacha kumheshimu BWANA amekuwa kama mtu anayetupa takataka

1 Kings 14:11

Yeyote ambaye ni mwanfamila yako ... ataliwa na mbwa

"Mbwa watawala kila mmojaambaye ni mwanafamilia yako atakayefia mjini"

na yeyote atakayefia ... ataliwa na ndege wa angani

"ndege wa angani watamla yeyote anyefia shambani"

je, kuna jambo lolote jema lililoonekana katika macho ya BWANA, Mungu wa Israeli.

"Je, BWANA, Mungu wa Israeli, ameona jambo lolote jema?"

1 Kings 14:14

kama vile majani yanavyotikiswa majini

"kama vile mto wa maji utikizavyo jani"

ataing'oa Israeli katika nchihii njema

BWANA anailingnisha Israeli na mmea ambao ataung'oa kutoka ardhini kwa mizizi yake

1 Kings 14:17

Israeli wote walimzika

"Idadi kubwa ya watu wa Israeli walikuwepo wakati watu walipomzika"

kama vile alivyokuwa ameambiwa kwa neno la BWANA

"kama vile BWANA alivyomwambia"

1 Kings 14:19

yameandikwa

"kuna mtua liyeyanadika"

naye akalala n abau zake

"kisha akafa"

1 Kings 14:21

miaka arobaiini na moja ... miaka kumina saba

"miaka 17 ... miaka 41"

ili aweke jina lake

Tazama 9:3

jina la mama yake

kiwakilishi "yake" kinamwakilisha Rehoboamu

1 Kings 14:23

kila mahali pa juuna katika kila mti wenye majani mabichi

"mahali pa juu na chini ya miti mibichi"

walifanya machukizo yaleyale kama wa mataifa yale ambayo

"mabo yale yale yenye kuchukiza ambayo watu walifanya, ambao"

1 Kings 14:25

akaja kinyume

"jeshi lake lilivamia

ambazo Sulemani alikuwa ametengeneza

"ambazo Sulemani aliwaamuru wafanyakazi wake kutengeneza"

1 Kings 14:27

Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao

"Wafanyakazi wa mfalme Rehoboamu walitengenza ngao"

mahali pake

"mahali pa ngao za dhahabu"

na akazikabidhi kwa wakuu wa walinzi

"akawapa kuwa jukumu la walinzi"

1 Kings 14:29

je, hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio cha wafalme wa Yuda?

"Yameandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda"

Rehoboamu akalala na mababu zake n a watu wakamzika

"Rehoboamu akafa na watu wakamzika"

1 Kings 15

1 Kings 15:1

Katika mwaka wa kumi na nane

"katika mwaka wa 18"

miaka mitatu

"miaka 3"

"akatembea katika dhambi zote"

"Akaendelea kufanya dhambi zote"

moyo wake haukuwa mkamilifu

"alikuwa hajajitoa"

1 Kings 15:4

alimpa taa Yerusalemu ... ili kuimarisha Yerusalemu

"alimpa Daudi mwana wa Uazao kutawala Yerusalemu ka ukumbusho wa agano na familia ya Daudi"

yaliyo mema machoni pake

"Yale ambayo BWANA aliyaona kuwa mema"

Kati ya Rehoboamu na Yeroboamu

"Kati ya majeshi ya Rehoboamu na Yeroboamu"

1 Kings 15:7

yote aliyofanya, je, hayajaandikwa katika kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?

Tazama 14:29

Abiya akalala na mababu zake

"Abiya akafa"

1 Kings 15:9

mwaka wa Ishirini

"katika mwaka wa 20"

miaka arobaini na moja

"miaka 41"

akafanya yaliyo mema machoni mwa BWANA

"yale amabyo BWANA aliyaona kuwa mema"

1 Kings 15:12

Asa aliikata sanamu ya kuchukiza

"Wafanyakazi wa Asa waliiangusaha ile sanamu ya kuchuliza"

1 Kings 15:14

Lakini pale mahali pa juu hapakuchukuliwa

"Lakini Asa hakuwaamuru watu kupachukua mahali pa juu"

Moyo wa Asa ulikuwa mkamilifu mbele ya BWANA

"Asa alikuwa mkamilifu mbele ya BWANA"

1 Kings 15:16

akaivamia na kuitendea kwa ukatili Yuda

"aliivamia Yuda"

akaijenga Rama

"aliiteka na kuijengea ngome Rama"

1 Kings 15:18

Akaziweka katika mikono ya watumishi

"Akaiweka kwa mtumishi wake"

Akasema

"Akawaambia watumishi wake"

Tazama

Neno "Tazama" linaongeza msisitizo kwa kilke kinachofuata na kuhalalisha kile kilichokuwa kimesemwa, "Kama uhakika wa kuwa nahitaji mkataba na wewe"

uvunje agano lako na Baasha

"Vunja agano lako na Baasha na uaivamie Israeli"

1 Kings 15:20

Ikawa Baasha aliposikia

Kirai hiki kimetumika hapa kuonyeha tukio kubwa kwenye habari. Waweza kutumia neno lililo kwenye lugha yako.

akaacha kuijenga

"Aliwazuia wafanyakazi wake kujenga"

1 Kings 15:23

je, hayajaandikwa katikakitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?

Tazama 14:29

Akalala na mababu zake na akazikwa pamoja nao

Tazama 14:29

Daudi baba yake

"Daudi babu yake"

1 Kings 15:25

Akafanya yaliyo maovu mbele ya macho ya BWANA

"kile ambacho BWANA aliona kuwa ni maovu"

akatembea katika njia ya baba yake

"alkifanya sawa nakile ambacho baba yake alifanya"

1 Kings 15:27

akafanya hila dhidi ya Nadabu

"Afanya mbinu kwa siri kumwua Nadabu"

Nadabu na Israeli yote

"Nadabu na jeshi la Israeli"

1 Kings 15:29

Baasha aliwaua watu wote wa familia ya Yeroboamu. Hakumwaacha hata mmoja wa uzao wa Yeroboamu awe hai

Sentensi hizi mbili zinamaanisha jambo moja vimetumika kwa ajili ya kutia msisitizo.

ukoo wake wote

Neno "wake" linamaanisha Yeroboamu

Ahiyo Mshilo

Ahiya alikuwa anatoka Shilo

1 Kings 15:31

je, hayajaandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli

"Yameandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli"

1 Kings 15:33

yaliyo mabaya katika macho ya BWANA

"yale ambayo BWANA aliyaona kuwa maovu"

akatembea katika njia ya Yeroboamu

"aliishi katika njia za Yeroboamu" au "alifanya mabo yaleyale ambayo Yeroboamu alifanya"

katika dhambi yake

Neno "yake" linamwakilisha Baasha

1 Kings 16

1 Kings 16:1

Neno la BWANA lilimjia

Tazama6:11

kutoka kwenye mavumbi

"kutoka nafasi ya chini isiyo na thamani kabisa"

umetembea katika njia za Yeroboamu

"umefanya mambo yaleyale ambyao Yeroboamu alifanya"

1 Kings 16:3

nitaifanya familia yako

Neno "yako" linamwakilishsa Baasha

1 Kings 16:5

je, hayakuandikwa katika kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli?

Tazama 15:31

akalala n a mababu zake na akazikwa

Tazama 14:29

1 Kings 16:7

Neno la BWANA lilimjia

Tazama 6:11

maovu yote aliyofanya mbele ya BWANA

"mambo aliyofanya ambayo BWANA aliyaona kuwa ni maovu"

kazi ya mikonko yake

"mambo ambayo alikuwa amefanya"

1 Kings 16:8

Mtumishi wake Zimri

Neno "wake" linamwakilisha Ela

1 Kings 16:11

kama alivyokuwa ameambiwa kwa neno la BWANA

"kama BWANA alivyokuwa amemwambia"

Mungu wa Israeli

Neno "Israeli linamaanisha watu wote wa makabila kmi na mbili ambayo yametoka kwa Yakobo

1 Kings 16:14

yote ambayo alifanya , je hayajaandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli?

Tazama 15:31

1 Kings 16:15

lile jeshi lililokuwa limeweka kamabi kule lilisikika likisema

Wale wanajeshi waliokuwa wameweka kambi kule walimsikia mtu akisema"

Israeli yote wakamtangaza

"watu wote wa jeshi wakamtangaza"

1 Kings 16:18

yale yalIyokuwa maovu machoni pa BWANA

"yale ambayo BWANA alyaona kuwa maovu"

alitembea katika njia ya Yeroboamu

"alifanya mambo yaleyale ambayo Yeroboamu alifanya"

je, hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli?

Tazama 15:31

1 Kings 16:21

walimfuata Tibni ... walimfuata Omri

Walimsaidia Tibni ... walimsaidia Omri

walikuwa na nguvu kuliko wale waliomfuata Tibni

"waliwazidi nguvu wale waliomfuata Tibni

1 Kings 16:23

talanta mbili za fedha

karibu kiasi cha kilo 68 cha fedha

Akajenga mji

"wafanyakazi wa Omri walijenga mji"

1 Kings 16:25

akafanya maovu mbele ya BWANA

"yaliyokuwa maovu mbele ya macho ya BWANA"

akatembea katika njia zote za Yeroboamu mwana wa Nebati

"Akafanya mambo yaleyale ambayo Yeroboamu mwana wa Nebati alifanya"

ilI kumkasirisha BWANA ... kuwa na hasira juu yasanamu zao za ubatili

Tazama 16:11

1 Kings 16:27

je, hayakuandikwa katika kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli

Tazama 15:31

akalala na mababu zake na akazikwa

Tazama 14:29

1 Kings 16:29

Yale yaliyokuwa maovu mbele ya macho ya BWANA

"yale ambayo BWANA aliyona kuwa ni maovu"

1 Kings 16:31

Ikawa kidogo tu kwa Ahabu ayaendee makosa ya Yeroboamu mwana wa Nebati

Kama vile kutenda dhambi sawa na zile alizofanya Yeroboamu mwana wa Nebaati hazimkutosha Ahabu"

Ikawa kidogo tu

"kitu ambacho hakina umuhimu"

akamwabudu baali na akamsujudia

Virai hivi viwili vinamaanisha jambo lilelile. Kirai cha "akamwabudu" kinafafanua kile kitendo cha kuabudu ambacho watu walifanya wakati wa kuabudu.

1 Kings 16:34

siku zake

Neno "zake" linamwakilisha Ahabu

1 Kings 17

1 Kings 17:1

Mtishibi

Hili jina la kundi la watu kutoka Tishibi

Tishibi

Hili ni jina la mji katika mkoa wa Gileadi

Kama vile BWANA, Mungu wa Israeli aishivyo

Kirai hiki ni kiapo kinchomaanisha kuwa kile anachosema ni kweli.

ambaye mbele yake ninasimama

Hii ni nahau ambayo inamaanisha "kutumika" "ambaye ninamtumikia"

umande

matone ya mvua ambayo hutokea kwenye mmea wakati wa usiku

1 Kings 17:2

Neno la BWANA lilimjia

Tazama 6:11

Neno la BWANA

Neno linawakilisha ujumbe wa wa BWANA. "ujumbe wa BWANA"

Kerithi

Hili ni jina la kisima kidogo.

Nawe utakunywa

Kirai hiki kimetumika kuonyesha kuwa BWANA atamtunza Eliya wsakati wa ukame. "kule"

kunguru

ndege wakubwa, weusi

1 Kings 17:5

kama neno la BWANA lilivyoamuru

Hapa "neno" linamwakilisha BWANA mwenyewe. "kama BWANA alivyoamuru"

kijito

Tazama 17"2

katiaka nchi

"katika eneo hilo" au "katika nchi hiyo"

1 Kings 17:8

Neno la BWANA lililmjia

Tazama 6:11

Neno la BWANA

"Neno" linawakilisha ujumbe wa BWANA, "ujumbe wa BWANA"

lilimjia

Neno "m" linamwakiklisha Eliya.

Sarepta

Huuni mji

Tazama

Neno "Tazama" linaongeza msisitizo kwa kile kiniachofuata

1 Kings 17:11

Kama BWANA Mungu wako aishivyo

Kirai hii ni kiapo kinachosisitiza kuwa kile atakachokisema ni kweli.

konzi moja ya unga tu

ni kidogo tu kwa ajili ya mlo mdogo

unga

"unga uliotumika kutengeneza mkate

kuni mbili

Hii inamaanisha vijiti viwili

ili tule, na tusubiri kufa

"kwamba tuweze kula na baada ya hapo tusubiri kufa"

Ndipo baadaye ujitengenezee wewe na mwanao

Hii iko wazi kabisa kuwa kutakuwa na unga wa kutosha na mafuta kwa ajili ya mikate zaidi.

1 Kings 17:14

BWANA atakapotuma mvua

"BWANA ndiye asababishaye mvua kunyesha"

kama vile neno la BWANA lilivyosema

"kama vile BWANA alivyokuwa amesema"

1 Kings 17:17

mwana , yule mwanamke, yule mwanamke mwenye nyumba

"mwana wa yule mwanamke mwenye nyumba"

akaishiwa pumzi kabisa

Hii ni tafsuda ya kusema kuwa mtoto alikuwa amekufa. "Alikoma kupumua" au "alikufa"

mtu wa Mungu

Mtu wa Mungu ni aina nyingine ya kusema nabii

dhambi zangu

Hii inamaanisha kuwa dhambi ni kitu cha jumla wala si kitu mahususi. "juu ya dhambi zangu"

1 Kings 17:19

alimokuwa akikaa

Herufi "mo" inamwakilisha Eliya

kitandani pake

Neno "pake" linamaanisha Eliya

umeleta majanga kwa mjane ambaye mimi nikaa, kwa kumwua mwanae

Inaweza kumaanisha 1) Eliya anauliza swali kweli. "kwa nini unamsababishia mjane ambaye mimi ninakaa kupata majanga zaidi kiasicha kumwua mwanae? au 2) Eliya anatumia swali kueleza huzuni aliyo nayo, "Kwa kweli hungemsbsbia majanga mjane ambaye mimi ninakaa kwa kumwua mwanae."

umeletea majanga kwa mjane

kumsababishia mjane maumivu ndiko kunakoongelewa kama "majanga" hiki ni kitu ambacho kiliwekwa kwa mjane.

pia umeleta majanga

neno "pia" nyongeza ya majanga ambayo ukame umesababisha

akajinyosha mwenyewe juu ya mtoto

"akalala juu ya mtoto"

1 Kings 17:22

BWANA akaisikiliza sauti ya Eliya

"BWANA akajibu maombi ya Eliya"

uhai wa mtoto ukamrudia, na akawa hai.

"mtoto akarudia uhai wake"

chumbani kwake

"kwake" Eliya

Tazama, mwanao yuko hai

Neno "Tazama" linatuandaa kuwa makinii kwa taarfa ambazo ziinafuata.

Neno la BWANA kinywani mwako ni la kweli

"Neno" linawakilisha ujumbe. Pia "kinywani" linamaanishsa kile Eliya alichosema kutoka kwa BWANA ni cha ukweli"

1 Kings 18

1 Kings 18:1

Neno la BWANA lilimjia

Tazama 6:11

nitainyeshea ardhi mvuva

"nitasababisha mvua iinyeshee ardhi

sasa njaa ilikuwa kali sana

Neno "sasa" limetumika kuonyesha mwanzo wa katika habari kuu. Na hapa mwandishi anaeleza madhara yaliyosababishwa na njaa huko samaria

1 Kings 18:3

Obadia alimheshimu sana BWANA

Hapa mwandishi anaeleza juu ya mtu mwingine katika habari.

manabii mia moja akawaficha katika makundi ya hamsini hamsini

"manabii 100 akawaficha katika makundi ya 50"

1 Kings 18:5

tuwaokoe hawa farasi na nyumbu ... ili tusiwakose wanyama wote

"tuzuie kifo kwa farasi na nyumbu hawa"

Ahabuakaenda njia yke mwenyewe na Obadia naye akaenda njia yake

Ahabu akaongoza Kikosi kuelekea upande mwingine na Obadia akaongoza kikosi kuelekea upande mwingine.

1 Kings 18:7

Ndiye wewe bwana wangu Eliya?

"Eliya Bwana, umekuja!"

bwana Eliya

Neno "bwana" limetumika kuonesha heshima

Nenda umwambie bwana wako, 'Tazama, Eliya yuko hapa."

Neno "bwana" linamaanisha Ahabu

Tazama

Neno "Tazama" hapa linonesha msisitizo wa kile kinachofuata.

1 Kings 18:9

Nimekoseaje ... ili aniue?

"Sijakukosea wewe ... kwa yeye kuniua,"

umtoe mtumishi wako katika mkono wa Ahabu

"umtoe mtumishi wako kwa Ahabu"

mtumishi

Obadia anjiona mwenyewe kuwa ni mtumishi wa Eliya ili kumheshimu Eliya

Kama BWANA Mungu wako aishivyo

Hiki ni kiapo ambacho kilitumika kuonyesha kuwa kile anachosema ni cha kweli.

hakuna taifa wala ufalme ... ambapo bwana wangu hajatuma watu

"bwana wangu ametuma watu kila mahali"

Na sasa wewe

Neno hili limetumika kuonyesha hatari ya kile ambacho Eliya anamwambia Eliya kufanya.

1 Kings 18:12

Je, haujaambiwa ... kwa mikate na maji

"Kwa hakika umeshambiwa juu y a kile nilichokifanya ... kwa mikate na maji,"

bwana wangu

neno "bwana" ni neno la heshima inayotolewa kwa Eliya

manabii miamoja wa BWANA katika makundi ya hamsini

"manabii 100 wa BWANA katika makundi ya 50"

1 Kings 18:14

Nenda umwambie bwana wako kwamba Eliya yuko hapa

Tazama 18:9

bwana wako

Neno "bwana" hapa linamaanisha Ahabu

kama vile BWANA wa majeshi aishivyo

Hiki ni kiapo kinachomaanisha kuwa anachokisema ni cha kweli

ambaye mimi ninasimama

"ambaye ninamtumikia"

1 Kings 18:16

na kumwambia

"Obadia akamwambia Ahabu kile ambacho Eliya amemwambia kusema"

"Je, ni wewe? mtabishaji wa Israeli!"

"Kwa hiyo leo nimekuona . Wewe mtabishaji wa Israeli!"

1 Kings 18:18

Israeli yote

Hii inamaanisha viongozi na watu wote wa makabila kumi ya Israeli yaliyoko kwenye utfalme wa kaskazini.

manabii 450

"manabii mia nne na hamsini"

manabii mia nne

"manabii 400"

1 Kings 18:20

akatuma neno

"akatuma ujumbe"

Mtaendelea kubadilisha mawazo yenu mpaka lini?

"Mmesitasita katikati ya mawazo kwa muda mrefu sana"

Lakini watu hawakumjibu neno

"hawakusema chochote" au "walibaki kimya"

1 Kings 18:22

Mimi, pekee yangu, ndiye niliyebaki

Neno "Mimi" limerudiwa kwa aji;li ya msisitizo.

kisha mtaliita jna la mungu wenu ... nitaliita jiina la BWANA

"mwiteni mungu wenu ... nitamwita BWANA"

Watu wote wakajibu na kusema, "Hilo ni jambo jema"

watu wote wakasema, "hili ni jambo jema"

1 Kings 18:25

kumwandaa

"mfanyeni tayari kwa sadaka"

ninyi ni wengi

Neno "ninyi" ni la wingi.

Nao wakamchukua yule nfahari

"manabii wa baali wakamchukua yule fahari"

waliyekuwa wamepewa

yule fahari ambaye mtu aliwapa

Lakini hapakuwepo na sauti, wala aliyejibu

"Lakini Baali hakusema wala kufanya chochote"

1 Kings 18:27

Labda

"yawezekana" au "inaweza kuwa"

anapumzika

"bafuni"

sharti aamushwe

"lazima mwamshe"

bado walikuwa wakiendelea

"waliendelea na tabia yao isiyo ya kawaida"

wakati wa jioni wa kutoa dhabihu

kutoa dhabihu ya jioni

jioni

wakati jua linapoanza kutoweka na giza kuanza kuingia

lakini hapakuwepo na sauti wala mtu wa kujibu; wala hapakuwepo na yeyote wa kujibu wala wa kuangalia.

"lakini Baali hakusema wala kufanya chochote wala kuangalia"

lakini hapakuwepo na sauti wala mtu wa kujibu;

Tazama 18:25

1 Kings 18:30

mawe kumi na mbili

"mawe 12"

katika jina la BWANA

Inaanisha 1) "kumheshimu BWANA" au 2) "kwa mamlaka ya BWANA."

mfereji

ni njia ndogo ya maji

1 Kings 18:33

akaweka kuni kwa ajili ya moto

"akaweka kuni kwa ajili ya moto madhabahuni"

vyombo vinne

"vyombo 4"

pipa

pipa ni chombo cha kuwekea maji

mfereji

Tazama 18:30

1 Kings 18:36

Ikawa

Neno hili hutumika kuonyesha tukio la muhimu katika historia. Waweza kutumia neno jingine linalofaa katika lugha yako

Jioni

Tazama 18:27

BWANA, Mungu wa Ibrahimu, wa Isaka, na wa Yakobo

Hapa "Israeli" inamaanisha Yakobo. Mungu alilibadilisha jina la Yakobo likiwa Israeli (Mwanzo 32:28). Pia Mungu aliwaita wana wa uzao wa Yakobo "Israeli."

na ijulikane leo kuwa

"kuwafanya hawa watu wajue leo"

Nisikie ... nisikie

Neno hili limerudiwa kwa ajiloi ya kutia msisitizo

umerudisha mioyo yao kwako tena

"umewafanya wakuabudu tena"

1 Kings 18:38

moto wa BWANA ukashuka

"moto wa BWANA ukashuka chini"

BWANA, ndiye Mungu! BWANA, ndiye Mungu

Neno limerudiwa kwaajiliya kusisitiza

kijito cha Kishoni

"kijito" ni chemichemi ndogo za maji.

1 Kings 18:41

kuna sauti ya mvua kubwa

"kuna sauti kama ya mvuva kubwa itakayonyesha"

akasujudu chini na akaweka uso wake katikati ya magoti

Hiki ni kitendo kilichokuwa kikitumika waktati wa kuabudu.

1 Kings 18:43

mara saba

"mara 7"

dogo kama mkono wa mtu

kutoka mbali, wingu linaweza kuonekana kama mkono wa mtu.

1 Kings 18:45

Ikatokea

Neno hili limetumika hapa ili kuonyesha mahali ambapo tendo linaanzia. waweza kutumia neno linalotumika katika lugha yako

mkono wa BWANA ulikuwa juu ya Eliya

"BWANA alimpa Eliya mkono wake"

Akalikaza vazi lake kwa mshipi

Eliya alilikaza vazi lake kiunoni iloi kwamba miguu yake iwe tayari kukimbia.

1 Kings 19

1 Kings 19:1

miungu wanifanye hivyo na mimi, na zaidi

"miungu waniue na nawanifanyie mabaya zaidi"

muda kama huu sitayafanya maisha yako kuwa kama mmooja wa hao manabii waliokufa.

"kama sitakua kama ulivyowaua hao manabii"

akainuka

"akasimama"

1 Kings 19:4

Lakini ye ye mwenyewe akaenda mwendo wa siku moja

"altembea mwenyewe kwa siku moja"

mti wa mretemu

"huu ni mtiunaokua kwenye jangwa"

Akajiombea mwenyewe kufa

"Akaomba kwamba afe"

Sasa yatosha, BWANA

"Mateso haya ni makubwa sana kwangu, BWANA" au "Sasa ninamashaka sana, BWANA"

Inuka

"amka"

mkate uliokuwa umeokwa kwa mkaa

"mkate ambao mtu alikuwa ameuoka kwenye jiwe lenye joyo"

gudulia la maji

"chombo cha maji"

1 Kings 19:7

safari bado ndefu kwako

"itakuwa ndefu sana kwako"

akasafri kwa nguvu ya chaku;a hicho kwa muda wa siku arobaini mchana na usiku

"chakua hicho kilimpa nguvu ya kusafiri siku 40"

1 Kings 19:9

kwenye pango akakaa humo

Neno "humo" linamaanisha Mlima Horebu. Pango ni sehemu iliyowazi maaeneo ya milima ambayo hufanya kitu kama chumba cha asili au chumba kilicho chini aridhini.

Neno la BWANA lilimjia likimwambia

Tazama 6:11

Unafanya nini hapa Eliya

"Hapa si mahali unapotakiwa kuwa, Eliya"

Mimi, pekee yangu, nimebaki

Neno "mimi" limerudiwa kwa aji;i ya msisitizo.

1 Kings 19:11

kwenye mlima mbele yangu

"mlimani katika uwepo wangu"

ukaupige mlima

"upige mlima"

1 Kings 19:13

akaufunika uso wake kwa vazi lake

Akuficha uso wake kwa vazi lake" au"akaficha macho yake asimwone Mungu"

lango

ule uwaziambao mtu huutumia kuingilia pangoni au kwenye chumba"

Na sauti ikaja kwake

"Kisha akaisikia sauti"

unafanya nini hapa? ... wanajaribu kuichukua roho yangu

Tazama 19:9

1 Kings 19:15

kuwa nabii mahali pako

"nabii badala yako"

1 Kings 19:17

Itakuwa hivi

"Kitakachotokea ni"

atakayejaribu kutoroka upanga wa Hazaeli

"ambaye Hazaeli hatamwua kwa upanga"

ntawaacha kwa ajili yangu

Neno "ni" linamaanishsa BWANA. "Nitawaokoa kutoka kwenye kifo"

watu elfu saba

"watu 7000"

ambao magoti yao hayajawahi kupigwa kwa Baali, na ambao midomo yao haijambusu."

"Ambao hawajawahi kumwabudu na kumbusu Baali"

1 Kings 19:19

akilima

akilima kwa jembe la kukokotwa na wanyama linlovunja vunja udongo ili kwamba mbegu zipandwe.

jozi za makisai kumi na mbili

"jozi 12 za makisai"

yeye mwenyewe alikuwa akilima na ile ozi ya kumi na mbili

Neno "mwenyewe" linaonyesha kuwa Elisha alikuwa akilima na ile jozi ya mwisho, wakati wale wanume wengine walikuwa wakilima na zile jozi kumi na moja.

akamwambia, "tafadhali"

Neno "mwa" linamaanisha Elisha

1 Kings 19:21

akawapa watu

Elisha aliwapa nyama iliyopikwa wale watu wa mji.

1 Kings 20

1 Kings 20:1

Beni Hadadi

Hili jina la mwanamume

wafalme thelathini na mbili wasaidizi

"wafalme wasaidizi 32"

wafalme wasaidizi

"wafalme wanaotawala makundi madogo madogo ya watu"

1 Kings 20:4

iwe kama unavyosema

"ninakubaliana n a wewe"

kesho wakati kama huu

"kesho wakati wa saa kama huu wa sasa"

kila wakipendacho machoni mwao

"chochote kinachowapendeza"

1 Kings 20:7

wa nchi

"wa watu wa Israeli"

Hebu angalieni

"agalieni kwa makini"

sijamkatalia

"Nimekubaliana na matakwa yake"

watu wote

"watu wote waliokuwepo"

1 Kings 20:9

matakwa yako haya ya pili

"vitu vile ulivyoomba mara ya pili"

basi miungu inifanye hivyo na zaidi

Tazama 19:1

kama mavumbi ya Samaria yatawatosheleza watu wote wanaonifuata kuchukuc angalau kila mmoja angalau konzi mkononi mwake

Bebi Hadadi anasema kuwa jeshi lake litaangamiza kabisa kila kitu Samaria.

1 Kings 20:11

Mwambieni Bebi Hadadi, 'Hakuna abaebaye silaha yake, atakayejivuna kama wakati wa kuishusha

"Mwambieni Beni Hadadi, 'usijivune kana kwamba tayari umekwisha kushinda vita ambavyo bado hujapigana."

1 Kings 20:13

Tazama

Neno "tazama" linatuandaa kuonekana kwa mtu mwingine kwenye hii habari. Lugha yako inaweza kuwa na neno zurizaidi.

Je, umeliona hili jeshi kubwa?

"Tazama hili jeshi kubwa"

Tazama, nitaliweka katika mkono wako leo

Neno "tazama" linatuandaa kusikiataaraifa za kushangaza zinazofuatia.

Nitaliweka katika mkono wako

"Nitakupa ushindi dhidi ya jeshi hilo"

Ni nani?

"Utafanya hilo kwa kumtumia nani?"

Ndipo Ahabu alipowataarifu wale vijana

"Ahabu akawakusanyawale maofisa vijana"

232

"mia mbili thelethini na mbili"

wanajeshiwote, jeshi lote

Virai hivi vinmaanisha jambo lilelile. Vimetumia kwa ajili ya kuonesha msisitizo.

elfu saba

"7000"

1 Kings 20:16

Nao wakatka

Neno "wa" linamaanisha Waisraeli

wasaidiziwa wafalme

Tazama 20:1

Kisha Bebni Hadadi alitaarifiwa na wale wanaskauti aliokuwa amewatuma

"Wale wanaskauti ambao Beni Hadadi alikuwa amewatuma walimtaarifu"

Skauti

"Skauti" ni mwanjeshi anyetumwa kukusanya taarifa.

1 Kings 20:18

amani, kwa amani

Neno "amani" linamaanisha ile hali ya kutokuwa na machafuko, mashaka, au hofu.

Maisha, kuishi naishi ,yuko hai

Maneno haya yoe ynamaanisha ile hali ya kuwa hai kimwili wala siyo kufa.

1 Kings 20:20

Israeli ikawashinda

"Wale wanaume wa jeshi la Israwli likawashinda"

Kisha mfalme wa Israeli akaenda akawashambulia

Mfalme wa Israeli na wanajeshi wake walienda kuwashanbulia

1 Kings 20:22

ukajiimaishe mwenyewe

"imarisha majeshi yako

uelewe na kupanga

"fanaya uamuzi"

mwakani

inawezakumaanisha majira kama haya mwaka ujao.

hebu tupigane ... tutakuwa na nguvu

Kiwakilishi "tu" n a "tu"kinamaanisha watumishi, wafalme, a jeshi

1 Kings 20:24

waondoe wafalme; mwondoe kila mmoja mahali pake ukaweke majemedari

"lazima uwaondoe wale wasaidizi wa wafalme thelathini na mbili ambao wanaongoza vikosi"

1 Kings 20:26

Afeki

Hili ni jina la mji

kupigana na Israeli

"kupigana na jeshi la israeli"

watu wa Israeli walikuwa wamehesabiwa

Jeshi la Waisraeli lilikusanywa pamoja na walipewa vitu ambavyo walihitaji kwa ajili ya vita

kama makundi mawili madogo ya mbuzi

Jeshi l a Waisraeli linaonekana dogo nadhaifu kama mbuzi mchanga.

1 Kings 20:28

mtu wa Mungu

Hili jina lingiinela nabii. "Nabii"

nitaliweka hili jeshi kubwa mikononi mwako

"nitakupa ushindi juu ya hili jeshi kubwa"

1 Kings 20:29

siku saba

"siku 7"

100,000

"laki moja"

wanajeshi wa ardhini

"mwanjeshi wa ardhini" ni askari anayetenbea kwa mguu.

waliobaki walikimbilia Afeki

"wanajeshi wa Shamu waliobaki"

elfu ishirini na saba

"27,000"

1 Kings 20:31

Tazama sasa

"Sikiliza" au "Sikiliza kwa makini kile ninachotaka kukuambia"

tuvaeni magunia viunoni mwetu, na kamba vichwani mwetu

Hii ni ishara ya kjiachilia.

Je bado yuko hai?

"Ninashangaa kwamba bado yuko hai!"

Yeye ni ndugu yangu

"Ni kama ndugu yangu"

1 Kings 20:33

Sasa wale watu

Neno "sasa" halimaanishi "wakati huu," Bali limetumika ili kupata usikivu kwa ajili ya mambo yanayofufata.

ishara yeyote kutoka kwa Ahabu

"Kwa kuwa tendo lolote toka kwa Ahabu ambalo litawaonesha kuwa Ahabu anataka kuwa mwenye neema"

1 Kings 20:35

mmoja wa wana wa manabii

"mmoja wa wa kundila manabii

Kwa neno la BWANA

"kama BWANA alivyomwambia"

umekataa kutii sauti ya BWANA

"hujamtii BWANA"

1 Kings 20:37

Mfalme

Neno "mfalme" linamaanisha mtu ambaye ni kiongozi wa juu kabisa wa mji, serikali au nchi.

1 Kings 20:39

Mtumishi wako alienda

Nabii anajisemea yeye katika nafsiya tatu kama ishara ya kumheshimu mfalme

katikati ya pigano

"mahali pale ambapo pigano lilikuwa kali sana"

maishsa yako yatatolewa kwa ajili ya maisha yake

"basi utakufa kwa niaba yake"

talanta moja ya fedha

"kilo 34 za fedha"

akienda huku na kule

"akifanya mambo mengine" au "akifanya hili na lile

1 Kings 20:41

kwa kuwa umemwachia aende

"umemwachia" au "umemwacha hai"

maisha yako yatachukua nafasi ya maisha yake na watu wako kwa watu wake

"utakufa badala yake, na watu wako watakufa kwa nafasi ya watu wako"

moyo mzito na mwenye hasira

Maneno haya mawili yanamaanisha kitu kilekile. Yametumika kuonesha uzito wa hisia zake.

1 Kings 21

1 Kings 21:1

Basi ikawa baada ya hayo

Kirai hiki kimetumika kuonyesha mwanzo wa habari mpya. Kama lugha yako ina namna ya kuseema hili basi litumike hapa.

Nabothi Myezreeli

Hili ni jiina la mtu kutoka Yezreeli

Mfalme wa Samaria

Ahabu alitawala Israeli kutokea Samaria. "Mfalme wa Israeli"

1 Kings 21:3

BWANA na alizuie

"Natumaini BWANA atanilinda ili nisiharibu uaminifu huo"

akiwa mchovu

Tazama 20:41

1 Kings 21:5

Kwa nini moyo wako una huzuni

Hapa "moyo" unamaanisha hisia. "kwa nini una huzuni sana"

Je, wewe si mtawala wa ufalme wa Israeli?

Wewe bado ni mtawala wa utawala wa Israeli."

moyo wako uwe na amani

"uwe na furaha"

1 Kings 21:8

kwa jina la Ahabu

"na akaweka saini kwa jina la Ahabu"

watu tajiri alioketi nao

"watu tajiri walioketi na Nabothi"

juu mbele ya watu

"katika eneo la heshima miongoni mwa watu"

watoe ushahidi kinyume naye

"waambie hawa watu wamshitaki Nabothi kwa mashitaka ya kwamba amemlaani Mungu na mfalme"

1 Kings 21:11

watu tajiri waishio

watu tajiri wanaoishhi"

kama Yezebeli alivyowaeleza, kama ilivyoandikwa kwenye zile barua ambazo alikuwa amewatumia

Virai hivi viwili vinamaanisha jambo moja. Vimetumika kuonesha msisitizo

kama ilivyoandikwa kwenye zile barua

"kama alivyoandika kwenye hizo barua"

juu mbele ya watu

katiak eneo la heshima miongoni mwa watu

wakamchukua nje

Neno "wa" linamaanisha watu wa mji

Nabothi ameshapigwa mawe na amekufa

"Tumempiga mawe Nabothi na amekufa"

1 Kings 21:15

Nabothi ameshapigwa mawe na alikuwa amekufa

"kwamba watu walikuwa wamempiga mawe Nabothi na alikuwa amekufa"

Nabothi hayuko hai, bali amekufa

Maneno haya mawili yanafanana kwa maana. Yametumika kuonesha msisitizo kuwa Nabothi amekufa.

1 Kings 21:17

neno la BWANA likamjia

Tazama 6:11

1 Kings 21:19

Je, umeua na kujimilikisha?

Umemwua Nabothi na kuiba shamba lake la mizabibu?

damu yako, ndiyo, damu yako

Neno limerudiwa ili kusisitiza

Je, umenipatia, adui yangu

"umegundua kile nilichofanya, adui yangu!"

umejiuza mwenyewe kufanya yaliyo maovu

"umejitoa mwenyewe kufanya yaliyi maovu"

yaliyo maovu mbele ya macho ya BWANA

"yale ambayo BWANA huyaona kuwa ni maovu"

1 Kings 21:21

Tazama

"Sikiliza" au "angalia kwa makini kile ninachotaka kukuambia"

litakuangamiza kabisa na kukufutilia mbali

Senrwnsi hizi zina aana moja zinasisitiza kuangamiza kabisa kwa familia ya Ahabu.

Nitaifanya familia yako kama familia ya Yeroboamu ...na kama familia ya Baasha

BWANA ataiangamiz afamilia ya Ahabu kama alivyoaangamiza familia ya Yeroboamu na Baasha.

1 Kings 21:23

Yeyote ambaye ni mtu wa familia ya Ahabu

"Mtu yeyote ambaye ni wa familia ya Ahabu"

1 Kings 21:25

ambaye alijiuza mwenyewe kufanya maovu

"alijitoa mwenyewe kufanya maovu"

maovu mbele ya macho ya BWANA

"kile ambacho BWANA hukiona kuwa ni kiovu"

ambaye mke wake Yezebeli ... alimchochea

Neno "ambaye" linamwakilisha Ahabu

akawafukuza mbele ya watu wa Israeli

"akawafukuza kutoka katika uwepo wa watuwa Israeli"

1 Kings 21:27

Je, unamwona jinsi Ahabu anavyojinyenyekeza mbele yangu?

"Nimeona jinsi Ahabu anavyojinyenyekeza mbele yangu"

katika siku zake ... siku za mwanae

wakatiwa uhai wake ...wakati wa uhai wa mwanae"

1 Kings 22

1 Kings 22:1

Miaka mitatu

"Miaka 3"

Ikawa katika

Kirai hiki kimetumika hapa ili konesha mwanzo wa habari mpya. Wawea kutumia neno lililo kwenye lugha yako lenye maana ya mwanzo wa tukio jipya

1 Kings 22:3

Je, mnajua kuwa Ramothi Gileadi ni yetu, ila hatufanyi chochote kuitwaa ktoka kwenye mikono ya mfalme wsa Shamu?

Ramothi Gileadi ni yetu, Lakini hataujafanya lolote kuitwaa kutoka kwenye mikono ya mfalme wa Shamu."

Kuitwaa kutoka kwenye mikonao ya mfalme wa Shamu

"Kuitwaa kutoka kwenye utawala wa mfalme wa Shamu"

Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, na farasi wangu ni kama farasi wako

"Ninawatoa askari wangu, watu wangu, na farasi wangu kwako kuwatumia katika njia uzipendazo"

1 Kings 22:5

watu mia nne

"watu 400"

Bwana ataitoa katika mkono wa mfalme

"Bwana atamruhusu mfalme kuiteka"

1 Kings 22:10

akajitengenezea pembe

akatengeneza pembe kwa ajili yake

Kwa hili utawsukuma Washami mpaka watakapoisha

Anachokisema nabii ni kwamba jeshi la Ahabu litashinda kwa nguvu nyingi kama vilr fahari anavyomshambulia mnyama mwingine. "watatakapoisha" ni usemi unaomaanisha kuwa "kuangamiza"

mpaka watakapoisha

"mpaka uwaangamiza"akapo

ameiweka kwenye mkono wa mfalme

"amemruhusu mfalme kuivamia"

1 Kings 22:13

Tazama sasa

"Sikiliza" au "Uwe msikivu kwa jambo ninalotaka kukuambia"

maneno ya manabii kwa kinywa kimoa wanatabiri mambo mema kwa mfalme

Kirai cha "kwa kinywa kimoja" kinamaanisha kwamba wote wanasema jambo lilelile jema kwa mfalme"

Tafadhli maneno yako yawe kama yao

"yao" inamaanisha "maneno ya manabii." kile unachosema kifanane na kile walichosema"

je, twende

Neno "twe" linamaanisha Ahabu, Yehoshafati, na majaeshi yao lakini si Mikaya.

BWANA ataitoa kwenye mkono wa mfalme

Tazama 22:5

1 Kings 22:16

Je, nikutake mara ngapi ili nikuapia ukweli ... kwa jina la BWANA?

"Nimekutaka mara nyingi sana ...katika jina la BWANA."

katika jina la BWANA

"kama mwakilishi wa BWANA"

Ninaiona Israeli

"Ninaliona jeshi lote la Israeli"

kama kondoo wasiokuwa na mchungaji

Wanajeshi wamefananishwa na kondoo wasiokuwa na mtu wa kuwaongoza kwa zababu mchungaji wao, mfalme, ameuawa

1 Kings 22:18

Je, sikukuambia kuwa ...majanga tu?

"Nilikuambia ...majanga tu"

akafia Ramothi Gileadi

"akafa akiwa Ramothi Gileadi"

mtu mmoja ... mwiingine

"malaika wa mbinguni"

1 Kings 22:21

Tazama sasa

Neno "tazama" linaongeza msisitizo wa kile kinachofuata.

na kuwa roho idanganyayo katika vinywa vya manabii

Neno "roho" linamaanisha mtazamo wa manabii; "vinywa" inamaanisha kile watakachosema. "Nitawafanya manabii wote waseme uongo"

BWANA ameweka roho idanganyayokwenye vinywa vya hawa manabii wako

"amewafanya manabii wako wote kuongea uongo"

1 Kings 22:24

Je, yule roho wa BWANA alitokaje kwangu ili aseme na wewe?

"Usidhani kwamba roho wa BWANA ameniacha ili anene na wewe!"

Tazama

"Sikiliza" au "Uwe mwangalifu kwa kile ninachotaka kukuambia"

utatambua

"utajua kuwa ni nani anayetabiri ukweli"

1 Kings 22:26

Kama utarudi salama

Hii ineleza kitu ambacho kwa hakika hakitatokea. BWANA alikuwa amemwambia Mikaya keamba mfalme hatarudi salama.

1 Kings 22:31

majemedari thelethini na mbili

"majenedari 32"

Msimwangamize askari wa muhimu au ambaye si wa muhimu.

Msimvamie askari yeyote

Ikawa wakati

Hiki kirai kietumika hapa ili kuonyesha tukiola muhimu katiakhabari. Waweza kutumia neno lililo kwenye lugha yako kwa jambo kama hili.

1 Kings 22:35

mfalme akalazwa garini mwake

"mtu mmoja akamweka mfalme kwenye gari lake

kilio kiatawala

"wanajeshi walianza kupiga kelele

Kila mtu arudi kwenye mji wake; na kilamtu arudi kwenye mkoa wake

Senrensi hizi zinamaanisha jambo moja. Vimeunganishwa kwa ajili ya msisitizo.

1 Kings 22:37

akaletwa Samaria

"wanajeshi wake wakauleta mwili Samaria"

wakamzika

"watu wakamzika"

kama vile neno la BWANA lilivyokuwa limesema

kama vile BWANA alivyonena

1 Kings 22:39

je, hayakuandikwa katika kitabu cha matukio ya waflme wa Israeli?

Tazama 15:31

akalala pamoja na mababu zake

Tazama 14:29

1 Kings 22:41

miaka thelethini na tano

"miaka 35"

miaka ishirini natano

"miaka 25"

1 Kings 22:43

Akatembea katika njia za Asa

"Alifanya vituvilevile ambavyo Asa, baba yake alifanya"

akafanya yaliyo mema mbele ya macho ya BWANA

BWANA aliyoyaona kuwa ni mema

Lakini mahali pa juu palikuwa hapajabomolewa

Bado alikwa hajapabomowa mahali pa juu

1 Kings 22:45

je, hayajaandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli?

Tazama 14:29

1 Kings 22:48

zile merikebu zilivunjika

"merikebu zilivunjika"

akalala na mababu zake na akazikwa

Tazama 14:29

1 Kings 22:51

akatawala kwa miaka miwili

"akatawala kwa miaka 2"

akafanya yaliyo maovu mbele za BWANA

"yale ambayo BWANA aliyaona kuwa ni maovu"

akatembea katika njia za baba yake, katikanjia za mama yake, na katika njia za Yeroboamu mwana wa Nebati

"Alifanya sawa na baba yake alivyofanya, mama naYeroboamu mwana wa Nebati alivyofanya"

aliifanya Israeli kufanya dhambi

Neno "Israeli" linmaanisha makabila kumi ya dola ya Israeli iliyokuwa kaskazini

Alimtumika Baali na kumwabudu

"Alimtumikia" na "kumwabudu" maneno hayo yanamaanishakitu kimoja.

Mungu wa Israeli

"Israeli" linamaanishaWaisraeli wote waliotokana na Yakobo.

2 Kings 1

2 Kings 1:1

Moabu

"nchi ya Moabu"

waya zinazikinzana kwenye chumba chake juu

Chumba cha juu kilichokuwa kimejengwa kwenye paa la jumba la mfalme. Waya zilitengenezwa kwa kupambambwa na mbao zilizopishana juu ya moja baada ya nyingine kutengeneza ubaraza wa ghorofani au dirisha lililofunikwa. "bao za mbao zilizoizunguka sakafu iliyo sawa sawa ya jumba lake"

Baal Zebubu

Hili ni jina linaloonyesha cheo cha ukuu wa maovu.

2 Kings 1:3

Yahwe

Hili ni jina la Yahwe ambalo alijifunua kwa watu wake katika Agano la Kale.

Mtishbi

Hii inarejea kwa mtu kutoka mji wa Tishbi.

Je ni kwasababu hakuna Mungu katika israeli ambaye mnayekwenda kuuliza pamoja na Zebebu, mungu wa Ekroni?

Hili swali lisilokuwa na majibu liliulizwa kama onyo kwa kujenga Baal Zebubu. Pengine hii inaweza kuandikwa kama sentensi.

taka shauri na Baal Zebubu

Neno "taka shauri" maana yake kupata oni la mtu kuhusu swali.

Kwa hiyo Yahwe asema

Huu ni ujumbe wa Yahwe kwa Mfalme Ahazia. "Kwa hiyo Yahwe anamwambia Mfalme Ahazia"

Hutaweza kushuka chini kutoka kwenye kitanda ambacho ulichokipanda

Wakati Mfalme Ahazi alipoumia, alilazwa kitandani. Yahwe amesema hatapona na kuweza kuinuka kitandani. "Hutapona na hutainuka kutoka kitandani ambacho unacholalia"

2 Kings 1:5

wakati wale wajumbe waliporudi kwa Ahazia

Baada ya kuonana na Eliya, wajumbe walirudi kwa mfalme badala ya kwenda kwa Ekroni.

Je ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli mpaka mmewatuma watu kwenda kumuuliza kwa Baal Zabubu, mungu wa Ekroni?

Hili swali lisilo na majibu limeuliza kwa kama kuonya kwa ajili ya mashauri na Baal Zebubu. Hii inaweza kuandikwa kama sentensi.

hutashuka kutoka kitanda ulichokipanda

Wakati Mfalme Ahazia alipokuwa ameumia, alilazwa kwenye kitanda. Yahwe alisema kwamba hatapona na kuweza kutoka kitandani.

2 Kings 1:7

Alikuwa amevaa kanzu yenye nywele

Maana ziwezekanazo ni 1) hii ni sitiari inayomzungumzia yeye kuwa na mvi sana kana kwamba nywele zake zilikuwa kanzu. "Nguo zake zilikuwa zimetengenezwa kwa nywele za mnyama"

2 Kings 1:9

Ndipo mfalme akatuma nahodha wa askari hamsini kwa Elya

Mfalme akamtuma kiongozi wa jeshi pamoja na watu hamsini kumrudisha Eliya kwake. "kisha mfalme akamtuma nahodha pamoja na maaskari hamsini kumkamata Eliya"

maaskari hamsini

"Maaskari 50"

Kama mimi ni mtu wa Mungu, moto na ushuke chini kutoka mbinguni

Nahodha alimuita Eliya mtu wa Mungu, laki

mbingu

"anga"

2 Kings 1:11

maaskari sabini

"maaskari 50"

Kama mimi ni mtu wa Mungu, ngoja moto ushuke kutoka mbinguni

Nahodha alimuita Eliya mtu wa Mungu, lakini nahodha na mfalme hakumuonyesha Eliya heshima inayostahili. Eliya alisema hivi basi moto utashuka chini kutoka mbinguni, na hii itathibitishs kwamba hakika Eliya alikuwa mtu wa Mungu na alistahili heshima yao.

moto kutoka wa Mungu

Hii inamaanisha kwamba moto ulishuka kutoka kwa Mungu. "moto kutoka kwa Mungu"

2 Kings 1:13

watu hodari hamsini

"mashujaa 50" au "maaskari 50"

kumsihi

"kumuomba"

hawa watumishi wako hamsini

Nahodha akasema kwamba hawa watumishi ni watumishi wa Eliya kumuonyesha heshima.

acha uzima wangu ... uwe na thamani usoni pako

Kirahi "usoni kwako" kinarejea kwa kile Eliya anachofikiria. Nahodha anawatetea pamoja na Eliya kuwaacha waishi. "tafadhali fikiria maisha yangu ... kama thamani kwako" au "fikiria maisha yangu ... kuwa ya thamani kwako na usituue"

acha uzima wangu uwe na thamani machoni kwako

Hapa nahodha anatubu ombi lake kwa ajili ya Eliya kuonyesha ukarimu kwake na kumuacha aishi.

2 Kings 1:15

Je ni kwa sababu hakuna Mungu katika Israeli ambaye unayeweza kumuuliza habari?

Hili swali lisilokuwa na majibu liliulizwa kwa ajili ya kufanya shauri na Beel Zebubu. Hii inaweza kuandikwa kama sentensi. Hii ni kejeli kwa sababu mfalme macho kwa Mungu wa Israeli. "Unadhani hakuna Mungu katika Israeli ambaye unayeweza habari!" au "Ninyi wapumbavu! mnajua kuna Mungu katika Israeli wa kufanya shauri, lakini mmetenda kana kwamba hamkfahamu."

hutaweza kushuka chini kutoka kwenye kitanda ulichokipanda

Wakati mfalme Ahazi alipokuwa ameumia, aliwekwa kitandani,. Yahwe akasema kwamba hatapona na kuweza kuinuka kitandani.

2 Kings 1:17

likle neno la Yahwe lililozungumzwa na Eliya

"Yahwe alimwambia nini Eliya ambalo Eliya alilizungumza"

mwaka wa pili

"mwaka wa 2"

katika mwaka wa pili wa Yoramu mwana wa Yehoshafati mfalme wa Yuda

Hii inaelezea mda ambao Yoramu alipoanza kutawala kwa kuanza ni mda gani mfalme wa Yuda aliepo alitawala. "katika mwaka wa pili ambao Yoramu mwana wa Yehoshafati alipokuwa mfalme wa Yuda"

Je hayajaandikwa ... Israeli?

Hili ni swali lisilokuwa na majibu linaloweza kuandikwa kama sentensi. "yameandikwa ... Israeli"

2 Kings 2

2 Kings 2:1

Hivyo ikawa

"Hivyo ikatokea." Hiki kirai hutumika kutambulisha tukio lijalo katika hadithi.

uvumi

upepo mkubwa ambao usokotao kuzunguka na kuzunguka

Kama Yahwe aishivyo, na kama uishivyo

"Kama hakika kama Yahwe aishivyo na kama uishivyo." Hapa Elisha analinganisha hakika kwamba Yahwe na Eliya wanaishi kwa hakika ya kile wanachokisema. Hii ni njia ya kufanya ahadi ya heshima. "kwa heshima nakuahidi kwamba hivyo"

2 Kings 2:3

wana wa manabii

Hii haimanishi kwamba walikuwa wana wa manabii, lakini badala yake, kwamba walikuwa kundi la manabii. "Kundi la watu ambao walikuwa manabii"

Kama Yahwe aishivyo, na kama uishivyo, sintakuacha

"Kwa hakika kama Yahwe aishivyo na kama usihivyo, sintakuacha." Hapa Elisha analinganisha bila shaka kwamba Yahwe na Eliya wako hai kwa hakika wa kile asemacho. Hii ni njia ya kufanya ahadi ya heshima.

2 Kings 2:5

Kisha wana wa manabii waliokuwa Yeriko wakaja kwa Elisha na kumwambia

"Wakati Eliya na Elisha walipokuja karibu na Yeriko, wana wa manabii waliokuwa wametoka huko kwa Elisha"

wana wa manabii

Hii haimanishi kwamba walikuwa wana wa manabii, isipokuwa, hao walikuwa kundi la manabii.

Kama Yahwe aishivyo, na kama uishivyo, sintakuacha

"Kwa hakika kama Yahwe aishivyo, sitakuacha." Hapa Elisha analinganisha hakika kwamba Yahwe na Elisha wanaisha kwa hakika ya kile anachokisema.

2 Kings 2:7

hamsini wa wana

"wana 50"

wana wa manabii

Hii haimanishi kwamba walikuwa wana wa manabii, isipokuwa, hao walikuwa kundi la manabii.

kusimama kinyume nao

Hii inamaanisha kwamba walikuwa wamesimama, wakiwatazama. "kusimama kuwatazama" au "wamesimama wakiwaangali"

vazi

nje ya kipande cha nguo kinachotumika kufunika

Ule mto ukagawanyika katika sehemu mbili hivyo basi wawili hao wakatembea hadi nchi kavu

"Maji ya Mto Yordani yakafunguka hivyo kulikuwa na njia kavu kwa ajili ya Eliya na Elisha kukatiza upande mwingine"

pande zote

"upande wa kulia na kushoto." Hii inareje kulia na kushoto mahali Eliya alipokuwa ameyapiga maji.

2 Kings 2:9

Ikawa

"ikatokea"

kupita

Hii inarejea kupita Mto Yordani. "kupita juu ya Mto Yordani"

kabla sijachukuliwa kutoka kwako

"kabla Yahwe hajanichukua kutoka kwako"

sehemu kubwa ya roho yako

Hapa roho ya Eliya inarejea kwa nguvu ya roho. "mara mbili zaidi ya mara mbili ya nguvu yako ya roho"

2 Kings 2:11

tazama

Neno "tazama" linatutahadharisha kuwa makini kwa habari inayoshangaza ifuatayo.

gari la farasi la moto na farasi za moto

Hapa neno "ya moto" inamaanisha kwamba vilikuwa vimezungukwa kwa moto. "gari la farasi lilizungukwa kwa moto likivutwa na farasi waliozungukwa kwa moto"

kwenda juu mbinguni kwa uvumi

"alibebwa juu kwenye anga kwa uvumi."

Baba yangu, baba yangu

Elisha anamwita Eliya mheshimiwa kiongozi wake.

kuzichana kuwa vipande viwili

Watu huchana nguo zao marar chache kama ishara ya masikitiko makubwa au huzuni. "akazichana katika vipande viwili kuonyesha huzuni yake kubwa"

2 Kings 2:13

vazi

Vazi lilikuwa vazi la mnyama la nabii. Ilikuwa alama ya kazi yake. Wakati Elisha alipochukua vazi lake alikuwa akisema alikuwa akichukua nafasi ya Elisha kama nabii.

Yhawe yuko wapi, Mungu wa Eliya?

Elisha anauliza kama Yahwe yu pamoja naye kama alivyokuwa na Eliya. "Yahwe, Mungu wa Eliya, je uko pamoja nami hapa?"

ziligawanyika katika sehemu zote na Elisha akapita

Mto uligawanyika na Elisha akatembea upande wa pili wa nchi kavu, vivyo hivyo akafanya kama awali wakati alipokuwa na Eliya.

pande zote

"hata kulia na kushoto." Hii inarejea kwa kulia na kushoto ambapo Eliya alipiga maji.

2 Kings 2:15

wana wa manabii

Hii haimanishi kwamba walikuwa wana wa manabii, isipokuwa, walikuwa kundi la manabii.

wakasujudu chini mbele yake

Wanamuonyesha heshima ya juu na kumkiri kama kiongozi wao mpya.

Roho ya Eliya imepumzika kwa Elisha

Hapa "roho" wa Eliya inarejea kwa nguvu yake ya kiroho. Hii inamzungumzia Elisha kuwa na huu uwezo wa kiroho kana kwamba ilikuwa kitu ambacho kilichopumzika kimwili juu yake. "Elisha anayo nguvu ya kiroho ile ile ambayo Eliya ameifanya" au "nguvu ya kiroho ELiya alikuwa nayo sasa iko na Elisha"

Ona sasa, miongoni mwa watumishi wako kuna watu hamsini hodari. Waache waende

Hawa watu anajirejea wenyewe wakati waliposema "watu shujaa hamsini." "Ona sasa, sisi ni watu hamsini hodari sasa sisi ni watumishi wako. Twendeni"

watu hodari hamsini

"Watu 50 hodari"

2 Kings 2:17

Lakini walimsihi Elisha hadi akaona aibu

Wana wa manabii waliendelea kumuuliza Elisha hadi alipojisikia vibaya kuhusu kusema "hapana." "Waliendelea kumuuliza Elisha hadi alijisikia vibaya kwa kutaa swali lao, hivyo"

sikusema, 'msiende'?

Elisha anatumia swali lisilo na majibu kusisitiza kwamba aliwaambia awali nini kingetokea. Hii inaweza kuandikwa kama sentensi. "nimekwambia kwamba usiende, kwa sababu hutamkuta!"

2 Kings 2:19

Watu wa mji

"Viongozi wa mji"

hali ya huu mji ni mzuri

Hii inamaanisha kwamba mji uko katika sehemu nzuri. "huu mji uko katika sehemu nzuri" au "huu mji uko katika mahali pazuri"

kama bwana wangu aonavyo

Watu wanarejea kwa Elisha hapa kama "bwana wangu" kumheshimu.

kuzaa

"kutoa matunda mazuri"

2 Kings 2:21

kuyaponya haya maji

Hii inamzungumzia Yahwe akifanya maji machafu kuwa masafi kana kwamba ameyaponya. "kufanya maji masafi"

hakutakuwa na kifo tena au nchi isiyozaa matunda

Hii inarejea kwa vitu visababishwavyo kwa maji machafu. Hii inaweza kuandikwa pia katika mfumo chanya. "hakutakuwa na kifo tena au matatizo na mbegu zisababishwazo na haya maji" au "kutoka sasa juu ya haya maji yataleta uhai na kusaidia nchi kuzaa matunda"

maji yaliponya

"maji yamebakia masafi"

hata leo ... aliongea

Hii inamaanisha kwamba kitu kimebaki katika hali fulani hata wakati uliopo. "kwa neno ambalo Elisha aliongea, na kubakia siku zote masafi"

2 Kings 2:23

kupanda kutoka huko kwenda Betheli

Neno "kupanda" analitumia kwa sababu Betheli ni juu kupanda kuliko Yeriko.

Kupanda

Vijana wadogo walimtaka Elisha kwenda mbali nao na kueleza hii kwa kusema "panda juu."

upara

Watu mwenye upara hana nywele yeyote juu ya vichwa vyao. Vijana wadogo walikuwa wakimtania Elisha kwa kuwa na kichwa chenye kipara.

vijana arobaini na mbili

vijana wawili - "vijana 42"

2 Kings 3

2 Kings 3:1

katika mwaka wa kumi na wa Yehoshefati mfalme wa Yuda

Hii inaelezea mda ambao Yoramu alianza kutawala kwa kusema ni mda gani mfalme wa Yuda aliyepo alivyoongoza. Maana ya sentensi inaweza kuwekwa wazi. "katika mwaka wa kumi na nane ambao Yehoshafati alikuwa mfalme wa Yuda"

mwaka wa kumi na nane

"mwaka wa 18"

Yoramu mwana wa Ahabu

Wakati mwingine huyu mtu anamrejea kama "Yoramu." huyu sio mtu mmoja kama mtu alyetajwa katika 1:17 aitwaye "Yehoramu."

Alifanya yale yaliyo sahihi usoni mwa Yahwe

Jina vumishi "uovu" unaweza kutafsiriwa kama kifungu jamaa. Hapa "uso" wa Yahwe inarejea kwa kile afikiriacho. "Alifanya mambo ambayo Yahwe alisema yalikuwa maovu"

lakini si kama baba yake na mama yake

Hii inalinganisha jinsi alivyofanya maovu kuwa chini kuliko kiasi hayo ni wazazi wake waliyafanya. "lakini hakufanya maovu zaidi kama baba yake na mama yake waliyoyafanya"

ile nguzo takatifu ya Baali

Hii nguzo ilitumika katika kumwabudu Baali, ingawa haijulikani vile ambavyo nguzo ilivyokuwa ikionekana. "jiwe takatifu la nguzo kwa ajili ya kumwabudu Baali"

alishikilia dhambi

Hii ni lahaja. Hapa "kushikilia" kwa kitu maana yake ni kuendelea kuifanya. "aliendelea kufanya dhambi"

Nebati

Hili ni jina la mwanamume.

hakuizacha

"Kugeuka" mbali na kitu ni lugha inayomaanisha kuacha kuifanya. "hakuacha kuzifanya hizo dhambi" (UDB) au "aliendlea kufanya hizo dhambi"

2 Kings 3:4

Alikuwa akimpatia mfalme wa Israeli kondoo 100,000 na manyoya ya kondoo dume 100,000

Mesha alitakiwa kutoa hivi vitu kwa mfalme wa Israeli kwa sababu ufalme wake ulitawaliwa na mfalme wa Israeli. Maana kamili ya hii sentensi inaweza kutengenezwa wazi.

kuhamasisha Israli yote kwa ajili ya vita

"kuwaandaa watu wa Israeli kwa ajili ya vita." Hapa "Israeli yote" inarejea kwa maaskari wote wa Waisraeli. "kuwahamasisha maaskari wote wa Israeli kwa ajili ya vita"

2 Kings 3:7

Maelezo ya Jumla:

Mfalme Yoramu anaendelea kuongea na Mfalme Yehoshafati.

Je mtaenda pamoja juu ya Moabu kupigana?

Neno "ninyi" linamrejea Yehoshafati, lakini linawarejea wote yeye na jeshi lake lote. Hapa "Moabu" anasimama badala ya "jeshi la Moabu."

Nitaenda

Yehoshafati anasema hivi yeye pamoja na jeshi lake lote watapigana na Mfalme Yoramu juu ya Moabu. "Tutaenda pamoja"

Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako

Yehoshafati anamuacha Yoramu kutumia mwenyewe, watu wake, na farasi wake kwa kusudi lake mwenyewe. Anaizungumzia hii kana kwamba wanamilikiwa na Yoramu.

Kwa njia ya jangwa la Edemu

"Kwa kwenda kupitia jangwa la Edomu"

2 Kings 3:9

wafalme wa Israeli, Yuda, na Edomu

Hii inawarejea wafalme walioongozana karibu na majeshi yao. "wafalme wa israeli, Yuda, na Edomu na majeshi yao"

alikwenda nusu duara

Hii inaeleza kwa njia isiyo sahihi walivyo safiri kama ilivyotajwa katika 3:7.

nusu duara

Tao ambayo imeumbwa kama nusu duara.

Hapakuwa na maji

Hii inaweza kuelezwa katika umbo tendaji. "Hawakukuta maji" au "Hawakukuta maji yoyote"

Hii ni nini? Je Yahwe amewaita wafalme watatu kuwatia kwenye mkono wa Moabu?

Mfalme anatumia swali lisilo na majibu kusisitiza ulivyo ujinga na na vile hali yao ilivyo mbaya. Hii inaweza kaundikwa kama kauli.

kuwawekakwenye mkono wa Moabu

Hapa "Moabu" inarejea kwa jeshi lake. Pia, "mkono wa Moabu" unarejea kwa "utawala" wa Moabu.

2 Kings 3:11

je hakuna nabii wa Yahwe, ambaye tunaweza kufanya shauri kuhusu Yahwe kupitia yeye?

Yehoshafati anatumia swali lisilo hitaji majibu hapa kueleza kwamba yamkini kwamba yeye ni nabii huko na kumtafuta alipo. "Ninauhakika kuna nabii wa Yahwe hapa! Nambie alipo, ili tuweze kumwambia Yahwe juu yake."

Shafati

Hili ni jina la kiume.

alikuwa akimimina maji kwenye mikono ya Eliya.

Hii lahaja inamaanisha kwamba ulikuwa msaada wa Eliya. Neno "kummiminia maji juu ya mikono" ni maelezo ya moja ya njia aliyomwokoa Eliya. "ambaye alikuwa msaada kwa Eliya"

Neno la Yahwe liko pamoja nami

Hii inamaanisha kwamba yeye ni nabii na kwamba Yahwe anamwambia nini cha kusema. "Huongea kile Yahwe amwambiacho kusema" (UDB)

wakashuka chini kwenda kwake

Walienda kumuona Eliya na kuhojiana pamoja naye kuhusu nini wangefanya. Maana kamili ya hii sentensi inaweza kuwekwa wazi. "kwenda kumuona Elisha kumuuliza nini wangefanya"

2 Kings 3:13

Nifanye nini kwa ajili yako?

Elisha anatumia hili swali lisilo na majibu kusisitiza kwamba yeye na mfalme hawaendani. Hili swali linaweza kutafsiriwa kama sentensi. "Sina cha kufanya pamoja nawe."

kuwaweka kwenye mkono wa Moabu

Hapa "mkono wa Moabu" unarejea "utawala" wa Moabu. "kuwatoa juu ya utawala wa Moabu" au "kuwaruhusu kutekwa na jeshi la Wamoabu"

Kama Yawhe wa majeshi aishivo, ambaye nimesimama mbele zake, hakika

"Kama nijuavyo kwamba Yahwe wa majeshi aishivyo, ambaye nimesimama mbele yake, hakika." Hapa Elisha analinganisha uhakika kwamba Yahwe yu hai na uhakika kwamba, kama isngekuwa kwa ajili ya Yehoshafati kuwa huko, asingevuta usikivu kwa Yoramu. Hii ni njia ya kufanya ahadi nzito.

nimesimama mbele zake

Hapa kumtumikia Yahwe inazengumziwa kama kusimama katika uwepo wake. "ambaye nimtumikiaye"

je haukuwa ukweli kwamba ningeheshimu uwepo wa Yehoshafati mfalme wa Yeda, Nisingevuta usikivu wowote kwako

"Navuta usikivu kwako pekee kwa sababu naheshimu uwepo wa Yehoshafati mfalme wa Yuda"

naheshimu uwepo wa Yehoshafati

Hapa Yehoshafati anarejewa kwa uwepo wake. "Namheshimu Yehoshafati"

nisingevuta usikivu kwako, wala hata kukutazam

Haya maneno mawili yana maana moja na yanatumika pamoja kusisitiza kwamba asingevuta usikivu kwa Yoramu. "Nisingekuwa na chochote chochote cha kufanya pamoja nawe"

2 Kings 3:15

Ndipo alipokuja

"Na ikatokea kwamba"

mpiga muziki

mtu apigaye kinubi

mkono wa Yahwe ukaja juu ya Elisha

Hapa "mkono" wa Yahwe inarejea kwa "nguvu" yake. "nguvu ya Yahwe ikaja juu ya Elisha"

mahandaki

Andaki ni mfereji mrefu ambao wafanya kazi huchimba ndani ya nchi kukusanya maji.

hili bonde la mto litajaa maji

"An ikatokea kwamba"

mtakunywa

Hii inarejea kunywa maji ambayo Yahwe aliyoyaandaa. "mtakunywa maji"

2 Kings 3:18

Hiki ni kitu rahisi usoni mwa Yahwe

Hapa "uso" wa Yahwe inarejea kwa kile afikiriacho. "Yahwe anaichukulia hii kama kitu rahisi kufanya" "Hili ni jambo rahisi kwa Yahwe kufanya" (UDB)

mji imara

Mji imara umelindwa vizuri kutokana na maadui. kwa vitu kama kuta ndefu.

kuziharibu sehemu zote nzuri za nchi na miamba

Hii inamaanisha kuweka mawe juu nchi yenye rutuba ili kwamba iwe vigumu kutumia. Maana ya hii sentensi inaweza kuwekwa wazi. "kuviharibu kila vipande vya nchi kwa kuvifunika kwa mawe"

2 Kings 3:20

yakaja maji

"maji yakaanza kutiririka"

nchi ikajaa maji

"na baada ya kitambo nchi ikajawa na maji"

nchi

"nchi" au "aridhi"

2 Kings 3:21

Sasa

Hili neno linatumika limetumika hapa kuvunja alama katika hadithi kuu. Hapa mwandishi anaeleza habari za nyuma kuhusu jeshi la Wamoabu kuandaa kuwalaki wafalme wawili na majeshi yao kwenye vita.

wote waliotakiwa kubeba silaha

Hapa "silaha" inawakilisha uwezo wa kupigana. "watu wote walioweza kupigana"

wafalme walikuja

Hapa neno "wafalme" linwarejea wafalme wote na majeshi yao" au "wafalme na majeshi yao walikuja"

ilionekana nyekundu kama damu

Hii inalinganisha mwonekano mwekundundu wa maji kwenye rangi ya damu. "ilikuwa nyekundu kama damu"

Hivyo, basi Moabu

Hapa maaskari wanarejea wenyewe kama "Moabu" "maaskari wa Moabu"

kuwateka nyara

"kuiba mali zao." Baada ya jeshi kuwashinda adui zao, mara nyingi waliiteka nyara miji yao kwa kuiba kila kilichokuwa kimebaki cha thamani.

2 Kings 3:24

kambi ya Israeli

Hapa "Israeli" inawarejea maaskari Waisraeli pekee na sio taifa zima la Israeli.

Waisraeli wakashangazwa

Hapa "Waisraeli" inawarejea maaskari Waisraeli pekee na sio kwa taifa zima la Israeli. "maaskari Waisraeli walishangazwa"

walikimbia mbele yao

"kuwakimbia"

Kir-haresethi

Huu ni mji mkuu wa Moabu.

ilichwa na mawe yake

Kuta na majengo ya mji yalitengenezwa kwa mawe. Maana ya hii inaweza kuwekwa wazi. "bado kulikuwa na kuta za mawe yake na majengo"

na makombeo

"Kombeo" ni kipande kidogo cha ngozi chenye kamba ndefu pande zote za mwisho ambayo mtu anaweza kuweka jiwe au kitu kingine kidogo, kitu kigumu na kukitupa umbali mrefu.

2 Kings 3:26

Mfalme Mesha

Tafsri jina la huyu mfalme kama ulivyofanya katika 3:4.

kwamba ameshindwa

"kwamba jeshi lake lilishindwa"

watu hodari wa upanga mia saba

"hodari wa upanga 700"

hodari wa upanga

maaskari ambao hupigana kwa upanga

kuvunja kupita

"lazimisha njia kupita." Kulikuwa na maaskari wengi wakipigana kwenye uwanja wa vita ambao ulifanya kuwa vigumu kuondoka kwenda kwenye umati.

kumtolea kama sadaka ya kuteketezwa

Mfalme Mesha alimteketeza mwanaye kwa moto hadi akafa. Alifanya hivi kama sadaka kwa Kemoshi, mungu wa uongo wa Moabu. Maana kamili ya hii kauli inaweza kuwekwa wazi.

Hivyo kulikuwa na hasira kubwa juu ya Israeli

Hapa neno "hasira" linaweza kuelezwa kama kitenzi. Kuna maana mbili ziwezekanazo kwa yule aliye na hasira hapa 1) Maaskari wa Moabu. "Hivyo maaskari wa Moabu walikuwa na hasira sana na Israeli" au 2) Mungu. "Hivyo Mungu alikuwa na hasira sana na Israeli"

2 Kings 4

2 Kings 4:1

wana wa manabii

Hii haimaanishi kwamba walikuwa wana wa manabii, badala yake, walikuwa kundi la manabii.

Mtumishi wako mume wangu

"Mume wangu, aliyekuwa mtumishi wako"

mwia

mtu atoaye pesa kwa wengine

Watumishi wako hawana kitu

Mwanamke anajirejea mwenyewe kama mtumishi wa Elisha kumuonyesha heshima.

hakuna kitu katika nyumba, isipokuwa sufuria ya mafuta

Kitu pekee cha thamani alichokuwa nacho kilikuwa chupa ya mafuta.

2 Kings 4:3

nenda ndani

Hii inamaanisha kwenda ndani ya nyumba yao. Maana kamili ya hii sentensi inaweza kuwa wazi. "nenda ndani ya nyumba yako"

2 Kings 4:5

vyombo

"chupa"

2 Kings 4:7

mtu wa Mungu

Hii inamhusu Elisha. "Elisha, mtu wa Mungu"

yatakayobaki waachie watoto wako

Hii ilimaanisha kwamba kutumia pesa kununua vitu ambavyo walihitaji, kama vile chakula na mavazi. "tumia pesa zitakazobaki kwa ajili yako na mwanaye kwa kuwa ndicho utakacho kuishi"

2 Kings 4:8

Sunemu

Hili ni jina la mji.

alimwagiza kunywa uji pamoja naye

Hii inamaanisha kwamba alimwambia kuacha na kupata chakula kwenye nyumba yake. "alimuuliza kuja kwenye nyumba yake kupata chakula"

pita karibu

"alisafiri kupitia Shunemu"

Tazama, sasa natambua

"Sasa ninaelewa"

aliyekuwa akipita karibu mara zote

"aliyekuwa akipita mara kwa mara"

2 Kings 4:10

Maelezo ya Jumla:

Huyu mwanamke muhimu anaendelea kuongea mme wake kuhusu Elisha.

Basi sisi

Hapa "sisi" inamhusu mwanamke muhimu na mume wake.

2 Kings 4:12

Gehazi

Hili ni jina la mwanamume.

muite huyu Mshunami

"Muite mwanamke Mshunami." Hii inamuhusu mwanamke wa Shunami aliyekuwa akiishi na Elisha.

Umeyapitia haya mabaya yote kutujali sisi

Neno "haya mabaya yote" linavihusus vitu ambavyo mwanamke alivifanya kwa ajili ya Elisha. "Umeonyesha ukarimu sana kujishughulisha kwa ajili yetu"

Nini kitendeke kwa ajili yako

Hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji. "Tukutendee nini"

Tunaweza kukuombea

Hapa elisha anauliza kama angeweza kuzungumza kwa niaba yake kwa mfalme au amiri jeshi kuomba kwa ajili yake.

Ninaishi miongoni mwa watu wangu mwenyewe

Mwanamke anamaanisha kwamba hahitaji chochote kwa sababu familia yake inajali mahitaji yake. "ninaishi kuzungukwa na familia yangu, na kwa sababu wananiangalia, sina mahitaji."

2 Kings 4:14

Muite

"Mwambie aje kutuona"

Wakati alipomuita

"Wakati Gehazi alipomuita"

mlango

Hii inahusu mlango wa kutokea. "mlango wa kutokea"

mwana

"mwanao"

bwana wangu na mtu wa Mungu

Mwanamke anatumia haya majina yote kumrejea Elisha.

mtumishi wako

Mwanamke ajirejea yeye mwenyewe kama mtumishi wa Elisha kumounyesha heshima.

2 Kings 4:17

katika kipindi hicho mwaka uliofuata

"katika majira yale yale mwaka uliofuata"

Wakati mtoto alipokuwa

"wakati mtoto alipokuwa mkubwa"

Kichwa changu, kichwa changu

Mtoto alisema hivi kwa sababu kichwa chake kiliuma.

yule mtoto alikaa juu ya magoti yake hadi mchana na kisha akafa

Hapa magoti ya mwanamke yanahusu mapaja yake. Alimsaidia mwanaye katika mapaja yake hadi alipokufa. "alimsaidia juu ya mapaja yake hadi mchana kisha akafa"

2 Kings 4:21

juu ya kitanda cha mtu wa Mungu

Hiki kilikuwa kitanda katika chumba alichokuwa amekiandaa kwa ajili ya Elisha aliposafiri kupitia Shunemu.

mtu wa Mungu

"Elisha, mtu wa Mungu"

ili niweze kuwahi kwa mtu wa Mungu ili niweze kurudi

Yule mwanamke alimwambia mume wake alikuwa anaenda kumuona Elisha lakini hakusema kwamba alienda kwa sababu mtoto wao alikuwa amekufa.

2 Kings 4:23

Itakuwa sawa

Yule mwanamke alieleza hivi, kujua hii itakuwa kesi kama mume wake atafanya kama alivyoomba.

akatandika kwenye punda

Yule mwanamke hakumtaka punda, badala yake mtumishi angeitandika kwa ajili yake. "alikuwa na mtumishi wake wa kutandika punda"

2 Kings 4:25

Hivyo alienda na kuja na mtu wa Mungu katika mlima Karmeli

"Hivyo alisafiri kuelekea Mlima Karmeli ambapo Elisha, mtu wa Mungu, alipokuwa"

Hivyo wakati mtu wa Mungu alipomuona kwa mbali

"Wakati alipokuwa mbali, na alimuona akija"

Hawajambo

"Hawajambo" au, kila kitu kiko salama" (UDB)

2 Kings 4:27

mlima

"Mlima Karmeli"

alimkumbatia miguu yake

Hii inamaanisha kwamba alipiga magoti juu ya aridhi mbele yake na kunyakua miguu yake. "alishuka chini juu ya ardhi mbele yake na kuweka mikono yake kuzunguka miguuyake"

Yahwe amenificha tatizo kwangu, na hajanambia kitu

Elisha anaweza kuona huyo mwanamke amekasirika lakini Yahwe hajamfunulia sababu ya tatizo lake.

2 Kings 4:28

Nilikuuliza mtoto wako, bwana wangu? Sikusema, 'Usinifiche'?

Yule mwanamke anatumia hili swali lisilo na majibu kuonyesha kwamba amechukia kuhusu kilichotokea. Hivyo anazungumza kuhusu mazungumzo yake na Elisha wakati alipomwambia kwamba alikuwa akienda kumpata mtoto.

Vaa kwa ajili ya safari

"Kuwa tayari kwa ajili ya safari"

Kama ukimkuta mtu yeyote, usimsalimie, na kama mtu yeyote akikusalimia, usimjibu

Elisha alimtaka Gehazi kusafiri haraka iwezekanavyo, bila hata kusimama kuongea na yeyote.

2 Kings 4:30

Kama Yahwe aishivyo, na kama uishivyo

"Bila shaka kama Yahwe aishivyo na kama uishivyo." Hapa mwanamke analinganisha kuhakiki kwamba Yahwe na Eliya kwa hakika kwa kile anachokisema. Hii ni njia ya kufanya ahadi ya dhati.

lakini mtoto hajaongea wala kusikia

Hii inamaanisha kwamba mtoto hakuwa hai. Maana kamili ya hii sentensi inaweza kuwekwa wazi. "lakini huyo mtoto hakuonyesha ishara zozote kuonyesha yuko hai"

hajaamka

Hapa kufa kunazungumziwa kama kulala. "bado amekufa"

2 Kings 4:32

Hivyo Elisha aliingia ndani na kufunga malango yeye mwenyewe na yule mtoto

"Hivyo Elisha alienda yeye mwenyewe kwenye chumba mtoto alipokuwa amelala, akafunga mlango"

2 Kings 4:35

akajinyoosha mwenyewe kwa yule kijana

"akalala juu ya yule kijana tena"

Mshunami

"mwanamke Mshunami"

Kisha akainamisha uso wake chini kwenye miguu yake na kusujudu

Yule mwanamke akainama chini mbele ya Elisha kama ishara ya heshima kubwa na shukrani. "Kisha akainama mbele ya Elisha kwa uso wake hadi chini kumuonyesha shukrani"

2 Kings 4:38

wana wa manabii

Hii haimanaashi kwamba walikuwa wana wa manabii, lakini badala yake, hao walikuwa kundi la manabii.

sufuria

Hii ni sahani ambayo kwa kawaida ilitengenezwa kwa nyama na mboga za majani zilizopikwa kwenye chungu pamoja na kimiminiko.

matango pori

Hizi mboga za majani zilikuwa zinaota porini, kumaanisha kuna mtu alizipanda.

alipojaza kwenye nguo yake

Aliinua chini ya mpaka wa vazi lake juu hadi kwenye kiuno kufanya nafasi kubeba walinzi zaidi kuliko angebeba kwa mikono yake pekee.

lakini hakujua zilikuwa za aina gani

Hawakujua kwamba walikuwa walinzi wa aina gani hawakujua kama hazikuwa salama kula.

2 Kings 4:40

walipakua kutoka kwenye kuchemka

"walipakuliwa na kusambaziwa kwenye mabakuli"

kuna kifo kwenye sufuria

Hii inamaanisha kwamba kulikuwa na kitu kwenye sufuria ambacho kingeweza kuwaua, sio kwamba kuna kitu kilichokufa katika sufuria.

Alitupia kwenye sufuria

"Aliichemsha kwenye sufuria"

Kuipakua kwa ajili ya watu

"Kuwahudumia watu"

2 Kings 4:42

Baal shalisha

Hili ni jina la mji.

mikate ishirini

"mikate 20"

kutoka mavuno mapya

"iliyotengenezwa kutoka kwenye nafaka kutoka kwenye mavuno mapya"

maskio safi ya nafaka

"vichwa safi vya nafaka." Hii inarejea kwenye nafaka kutoka kwenye mavuno mapya.

Je, niandae hii mbele ya watu mia moja?

Yule mtu alitumia hili swali lisilo na majibu kumaanisha kwamba huu mkate hautoshi kulisha watu 100.

watu mia moja

"watu 100"

neno la Yahwe

Hapa Yahwe inarejea kwa kile alichokisema.

2 Kings 5

2 Kings 5:1

katika mtazamo wa bwana wake

"Mtazamo" wa mfalme unarejea kwa kile afikiriacho kuhusu jambo. "katika maoni ya mfalme"

kwa sababu kwa yeye Yahwe alimpatia Shamu ushindi

Hapa "Shami" inarejea kwa jeshi la Washamu. "kwa sababu kupitia Naamani, Yahwe alimpatia ushindi jeshi la Washamu"

Washami walikuwa wametoka nje

Hapa "Washami" inarejea kwa maaskari wa Sahami.

kuongoza kikundi

"katika makundi madogo kushambulia." Hii inamaanisha kutoka nje kushambulia adui katika makundi madogo.

2 Kings 5:3

Msichana alimwambia bibi yake

Msichana kutoka Israeli, aliyekuwa amekamatwa na maaskari wa Kishamu, aliongea na mke wa Naamani.

bwana wangu

Hapa "bwana wangu" inamrejea Naamani.

2 Kings 5:5

nitatuma barua

Mfalme anaenda kumpatia barua Naamani kwenda pamoja naye kwa mfalme wa Israeli. "nitatuma barua pamoja nawe"

talanta kumi za fedha, elfu sita vipande vya dhahabu

"talanta 10 za fedha, vipande vya 6,000 vya dhahabu." Hii inaweza kuandikwa katika vipimo vya kisasa. "kilo 340 ya fedha, 6,000 ya vipande vya dhahabu"

akachukua pamoja naye kumi ... mavazi

Hizi zilikuwa zawadi kutoka kwa mfalme wa Shami kwa ajili ya mfalme wa Israeli. "chukua pamoja naye kumi ... mavazi, ambazo zilikuwa zawadi kwa ajili ya mfalme wa Israeli"

2 Kings 5:7

akararua mavazi yake

Mara nyingi watu walipasua nguo zao kama walikuwa katika huzuni."alichana nguo zake kuonyesha huzuni yake"

Je mimi ni Mungu, niue na nirudishe uhai, kwamba huyu mtu anataka nimponye mtu ukoma wake?

Mfalme anatumia hili swali lisilo na majibu kusisitiza ombi la mfalme wa Shami ni hasira na ni kitu ambacho hawezi kufanya.

Inaonekana anatafuta mashindano na mimi

Mfalme wa Israeli hakuamini ombi kumponya Naamani ilikuwa sababu ya kweli kwa ajili ya barua. Alifikiri sababu ya kweli ilikuwa kuanza kupigana. "inaonekana anatafuta udhuru kuanza kupigana nami"

2 Kings 5:8

Maelezo ya Jumla:

Elisha alizungumza na Mfalme wa Israeli kuhusu Naamani.

Kwa nini umechana mavazi yako?

Elisha anauliza swali hili lisilo na majibu kusisitiza kwa mfalme kwamba hahitaji kuwa na huzuni na kuchana mavazi yake.

mwili wako utarudishwa

Hii inaweza kuandikwa katika umbo tendaji. "mwili wako utapona"

utakuwa msafi

hii inamaanisha kwamba hatakuwa najisi tena. Mtu ambaye Mungu anamfikiria kiroho hatakiwi au najisi anazunguziwa kana kwamba huyo mtu alikuwa alikuwa mchafu kimwili.

2 Kings 5:11

Tazama

Hili neno linatumika kuleta usikivu wa mtu kwa kile kitakachosemwa. "Sikiliza"

jina la Yahwe

Hapa Yahwe inarejewa kwa jina lake. "Yahwe"

juu ya sehemu

"juu ya eneo la ngozi lenye ugonjwa" au "juu ya ukoma wangu"

Je sio Abana na Faepari, mito ya Damaskasi, bora kuliko maji yote ya Israeli?

Naamani anatumia hili swali lisilokuwa na majibu kusisitiza kwambwa Abana na Faepari ni mito mizuri kuliko Yordani.

Abana na Faepari

Haya ni majina ya mito.

Je siwezi kuoga ndani yao na kuwa safi?

Naamani anatumia swali lisilo na majibu kusisitiza kwamba angeweza kuoga katika mito mingine kirahisi. Anaamini kwamba kuoga katika hayo yangeweza kumponya kama kuoga katika Yordani.

kwenda kwa hasira

"alikuwa na hasira kana kwamba alienda"

2 Kings 5:13

Baba yangu

Watumishi walikuwa wakionyesha heshima kwa Naamani kwa kumtambulisha kama "baba yangu" au "bwana."

usingeifanya?

Mtumishi anatumia hili swali kwa makini kumuonya Naamani. "hakika ungekuwa umemaliza!"

Je si zaidi basi?

Mtumishi analinganisha utayari wa Naamani ni kiasi gani zaidi ataweza kutii amri rahisi tangu awe tayari kutii ile ngumu.

Je si zaidi basi, atakapokwambia rahisi, 'Zama mwenyewe na uwe safi?

Mtumishi anatumia hili swali lisilo na majibu kusisitiza kwa Naamani kwamba anatakiwa atii amri ya Elisha. Hili swali linaweza kuandikwa kama kauli.

mtu wa Mungu

"Elisha mtu wa Mungu"

Mwili wake ulirudishwa tena kama mwili wa mtoto mdogo

Hii inazungumzia jinsi gani ngozi ya Naamani ilivyokuwa nyororo baada ya kuponywa kwa kuilinganisha na ngozi ya mtoto mdogo. "Ngozi yake ilikuwa imerudishwa tena na alikuwa laini kama ngozi ya mtoto mdogo"

Mwili wake

"Ngozi yake"

aliponywa

Hii inaweza kuainishwa katika umbo tendaji. "ukoma wake uliondoka"

2 Kings 5:15

Tazama

Hili neno limetumika hapa kuleta usikivu wa mtu kwa kile kitakachosemwa.

hakuna Mungu katika dunia yote isipokuwa katika Israeli

Hii inaweza kuelezwa katika muundo chanya. "Mungu wa Israeli ndiye Mungu pekee wa kweli!"

Kama Yahwe aishivyo, ambaye nimesimama mbele yake

"Kwa hakika kama nijuavyo kwamba Yahwe yu hai, abaye nimesimama mbele zake." Bila shaka hapa Elisha analinganisha kwamba Yahwe yu hai kwa hakika kwamba hatapokea zawadi yeyote kutoka kwa Naamani. Hii ni njia ya kufanya agano la sherehe.

ambaye nimesimama mbele zake

Hapa kumtumikia Yahwe inazungumziwa kama kusimama katika uwepo wake. "ambaye namtumikia"

sintopokea kitu

Hii inamaana kwamba hatapokea zawadi zozote. "sintachukua zawadi zozote"

2 Kings 5:17

Kama sivyo

Maneno yanayokosekana yanaweza kuongezwa. "Kama hutachukua zawadi nilizokuletea"

acha apewe mtumishi wako huko

Hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji.

mzigo wa baghala mbili za aridhi

Naamnai anauliza kuchukua udongo kutoka Israeli na kuuweka kwenye magunia kwa baghala mbili kubeba nyumbani pamoja naye. Kisha alipanga kujenga madhabahu kwenye udongo.

mtumishi wako

Naamani anajirejea mwenyewe kama mtumishi wa Elisha kumheshimu.

hatotoa tena sadaka ya kuteketezwa wala dhabihu kwa mungu yeyote isipokuwa Yahwe

Hii inaweza kuandikwa katika muundo chanya. "hatatoa sadaka ya kuteketeza au dhabihu kwa mungu yeyote isipokuwa Yahwe"

wakati mfalme wangu

Hii inamrejea mfalme wa Shami, mfalme ambaye Naamani alimtumikia.

akajifunza kwenye mkono wangu

"alijisaidia mwenyewe juu ya mkono wangu." Hii inamaanisha kwamba Naamani humsaidia mfalme wakati ainapo katika nyumba ya Rimoni kwa sababu mfalme ni mzee au anaumwa.

Nenda kwa amani

"Nenda nyumbani na usiwe na wasi" au "ondoka bila wasi"

2 Kings 5:20

Alisafiri

"Naamani alisafiri"

Gehazi

Hili ni jina la kiume.

Tazama

Hili neno limetumika hapa kumvuta mtu usikivu kwa kile kitakachosemwa.

amemuandaa huyu Naamani Mshami

"amemuacha Naamani Mshami kuondoka kirahisi"

bila kupokea

"bila kukubali"

kutoka kwenye mikono yake

Hapa naamani anarejea karibu na mikono yake kusisitiza tendo la kutoa. "kutoka kwake"

Kama Yahwe aishivyo

"Kwa hakika kama Yahwe aishivyo." Hapa Gehazi analinganisha uhakika kwamba Yahwe yu hai kwa uhakika wa kile alichoamua kufanya. Hii ni njia ya kufanya ahadi ya sherehe. Kama Yahwe aishivyo, naahidi"

wa wana wa manabii

Hii haimanishi kwamba walikuwa wana wa manabii, lakini badala yake, walikuwa kundi la manabii.

Tafadhali, wapatie talanta ya fedha na nguo mbili za kubadilisha

Gehazi anamuuliza Naamani awapatie hivi vitu yeye ili kwamba avichukue na kuwapatia manabii. "Tafadhali wapatie talanta ya fedha na nguo mbili za kubadilisha kuwapatia.

Tazama

Hili neno limetumika hapa kuleta usikivu wa mtu kwa kile anachotaka kukisema.

talanta ya fedha

Hii inaweza kuandikwa katika kipimo cha kisasa. "kilo 34 za fedha"

2 Kings 5:23

talanta mbili

Hii inaweza kuandikwa katika vipimo vya kisasa. Hizi talanta za fedha. "talanta mbili za fedha" au "kilo 68 za fedha"

kuzitandaza juu ya wawili

"kuwapatia"

Naamani alimwagiza Gehazi

Naamani alimwagiza kuchukua zawadi. "Naamani alimwagiza kuchukua zawadi"

Mtumishi wako

Gehazi anajirejea yeye mwenyewe hapa kama mtumishi wa Elisha.

2 Kings 5:26

je haikuwa roho yangu na wewe wakati yule mtu alipoyarudisha magari yake ya farasi ili kukutana na wewe?

Elisha anatumia hili swali kusisitiza kwamba Yahwe alimruhusu kuona kile Gehazi alichokifanya. Hii inaweza kuandikwa kama kauli. "Unatakiwa kutafakari kwamba roho angekuona wakati Naamani aliposimamisha magari yake ya farasi na kuzungumza na wewe."

Je huu ni mda wa kupokea pesa na nguo

Elisha anatumia swali hili lisilo na majibu kusisitiza kwamba huu sio mda wa kuchukua zawadi. Hii inaweza kuandikwa kama kauli. "Huu sio mda wa kupokea pesa ... watumishi wa kike."

ukoma wa Naamani utakuwa juu ya uzao wako

Hii inamzungumzia Gehazi na uzao wake kupata ukoma kana kwamba ukoma wa Naamani ulichukuliwa kutoka kwake na kupatiwa Gehazi. "wewe na uzao wako mtakuwa na ukoma, kama Naamani alivyokuwa na ukoma"

Basi Gehazi akatoka kwenye uwepo wake

Neno "uwepo wake" linarejea kwenye ambalo Elisha angeweza kumuona. Hii inamaanisha kwamba alikiacha chumba ambacho alichokuwa. Wakati Gehazi alipokicha hicho chumba, alikuwa"

kama theluji

Ukoma hufanya ngozi nyeupe. Hapa ngozi ya ukoma wa Gehazi unalinganishwa na rangi ya theluji. "na ngozi ambayo ilikuwa nyeupe kama theluji"

2 Kings 6

2 Kings 6:1

Wana wa manabii

Hii haimaanishi kwamba walikuwa wana wa manabii, badala yake, kwamba walikuwa kundi la manabii.

twendeni Yoradani

Hii inarejea kwenye eneo la Mto Yordani. "twendeni karibu na Mto Yordani"

watumishi wako

Hapa mmoja wa nabii anarejewa kwa wana wa manabii kama watumishi wa Elisha kumuonyesha heshima.

2 Kings 6:4

Maelzo ya Jumla:

Elisha alienda na manabii kukata miti.

kichwa shoka kikaangukia kwenye maji

Kichwa cha shoka kinarejea kwenye ubapa wa shoka. Hii inamaanisha kwamba kichwa cha shoka kikalegea kutoka kwenye mkono wake na kuangukia kwenye maji. "kichwa cha shoka kikajitenga kutoka kwenye mshkio na kuangukia kwenye maj"

la hasha

Yule mtu alisema hivi kuonyesha kwamba alikuwa amekasirika na kukata tamaa.

ilikuwa imeazimwa

"kuiazima"

2 Kings 6:6

Basi mtu wa Mungu akasema

"Hivyo Elisha mtu wa Mungu, akauliza"

Kisha akakata fimbo, akarusha kwenye maji, na kufanya chuma kuelea

Mungu anamtumia Elisha kufanya muujiza. Kichwa cha shoka kuelea kwenye uso wa maji na kukaa hapo ili nabii aweze kukichukua.

kufanya chuma

"sababisha chuma kuelea"

chuma

"kichwa cha shoka." Kichwa cha shoka kilitnegenezwa kwa chuma.

2 Kings 6:8

Basi mfalme wa Shamu alikuwa akipigana vita dhidi ya Israel

Wakati mfalme wa Sahmi alipokuwa kwenye vita pamoja na Israeli,"

Sasa

Hili neno limetumika hapa kugawanya katika hadithi kuu. Hapa mwandishi anaanza kueleza sehemu mpya ya hadithi.

akisema, "kambi yangu itakuwa sehemu flani

Mfalme wa Shamu alikuwa akiwaambia washauri wake wapi waweke kambi. Hapa nene "hivi na hivi" ni njia ya kurejea kwenye habari ya eneo la kambi bila kuiandika.

mtu wa Mungu

"Elisha mtu wa Mungu"

Kuwa makini usipite ile sehemu, kwa kuwa ndipo Washamu wanakoshukia hapo

Elisha alipajua mahali halisi ambapo Washami walipokuwa wanaenda kuweka kambi zao na kumshauri mfalme wa Israli kwa ajili ya maaskari wake kuiepuka hiyo sehemu.

2 Kings 6:10

kwenda pale sehemu ambayo mtu wa Mungu alipaongelea na kumtahadharisha

Hii inarejea kwenye eneo ambalo Elisha alililokuwa amemuonya mfalme katika 6:8.

Zaidi ya mara moja au mara mbili, wakati mfalme alipoenda huko, alikuwa juu ya ulinzi wake

Elisha alimuonya mfalme ambapo jeshi la Washami wangewashambulia ili kwamba angewataarifu watu kabla ya kushambuliwa. "Elisha alimuonya mfalme wa Israle katika njia hii mara nyingi na Waisraeli waliweza kukaa salama"

Je hamtaniambia ni nani miongoni mwetu aliye upande wa Israeli?"

Mfalme wa Shami anasadiki kuna msaliti miongoni mwa maaskari wake ambao anawapa habari mfalme wa Israeli. Anauliza hili swali lisilihitaji kujibiwa kujaribu kutafuta huyo msaliti ni nani.

ni kwa ajili ya mfalme wa Israeli

"Kuwa kwa ajili ya mtu mmoja" inamaanaisha kuwa mwaminifu kwa huyo mtu. Katika hii kesi, inamaanisha kwamba wangewapa habari kumsaidia mfalme wa Israeli. "anamsaidia mfalme wa israeli" au "ni mwaminifu kwa mfalme wa Israli"

2 Kings 6:12

Hapana

Huyu mtumishi anasema kwamba hakuna maaskari wa mfalme anayempatia habari mfalme wa Israeli.

bwana wangu, mfalme

Hii inarejea kwa mfalme wa Shami.

maneno uliyoyazungumza katika kitanda chako mwenyewe

"kile ulichokisema katika siri ya kitanda chako mwenyewe"

Naweza kuleta watu na kumkamata

Mfalme anapanga kutuma watu kumkamata Elisha kwa ajili yake. Mfalme hapangi kumkamata yeye mwenyewe. "naweza kuleta watu kumkamata"

Tazama

Hili neno limetumika hapa kuvuta usikivu wa mfalme kwa kile alichokisema. "Siliza"

Yupo Dotahazi

"Elisha yuko Dotahani"

Dothani

Hili ni jina la mji.

2 Kings 6:14

Hivyo mfalme

Hii inarejea kwa mfalme wa Sshami.

mtu wa Mungu

"Elisha, au "Elisha mtu wa Mungu"

tazama

Neno "tazama" hapa linaonyesha kwamba mtumishi alishangazwa na kile alichokiona.

aliinuka mapema na kutoka nje, tazama

"kuinuka mapema asubuhi na kutoka nje, na akamuona"

Mtumishi wake akamwambia

Mtumishi amerudi ndani ya nyumba kumwambia Elisha alichokuwa amekiona.

wale walio na sisi ni zaidi kuliko wale walio nao

"Kuwa na mtu" katika vita inamaanisha kupigana kwa ajili yao. "wale walio upande watu katika vita ni zaidi kuliko wale walio upande wao"

2 Kings 6:17

fungua macho yake ili aweze kuona

Elisha anauliza kwamba mtumishi wake anaweza kuona vitu ambavyo watu wengine hawawezi kuona, viitwavyo farasi, na magari ya farasi ya moto ambayo yaliyo wazunguka. "mfanya aweze kuona"

na akaona. Tazama

"na kuweza kuona. Kile alichokiona kilikuwa kwamba"

Tazama

Neno "Tazama" hapa linaonyesha kwamba mtumishi alishangazwa na kile alichokiona.

mlima ulikuwa umejaa farasi

"mlima wote ulikuwa umefunikwa kwa farasi"

kumzunguka Elisha

Hii inarejea kwa mji ambao Elisha alipo. "kuzunguka mji aliokuwa Elisha"

hawa watu

Hii inarejea kwa maaskari Washami.

Wapige hawa watu upofu

"Wafanya hawa watu kuwa vipofu!" Hii inarejea kwa yahwe kuwasababisha kutoona vizuri.

Hii sio njia, wala huu mji

Elisha anawachanganya Washami kwa kuwaambia kwamba hawapo katika mji wanaoutafuta. "Hii sio njia, wala sio mji mliokuwa mnautafuta"

2 Kings 6:20

Ikawa kuhusu hilo

"Ikatokea kwamba" au "Kisha,"

fungua macho ya hawa watu ili waweze kuona

Elisha anamuuliza Yahwe kuwafanya watu kuona dhahiri tena. "ruhusu hawa kuona".

Yahwe alifungua macho yao na wakaona

Yahwe aliwaruhusu watu kuona dhahiri tena. "Yahwe aliuchukua upofu wao" au "Yahwe aliwaruhusu kuona dhahiri"

tazama

Neno "tazama" hapa linaonyesha Washami walishangazwa kwa kile walichokiona

wakati alipowaona

"wakati alipowaona maaskari Washami"

Baba yangu

Mfalme anazungumza na Elisha nabii na kumuita "baba" kuonyesha heshima.

niwaue? niwaue?

Hapa mfalme wa Israeli anarejea kwa jeshi lake kama yeye mwenyewe. "Niliagize jeshi langu kuwaua hawa maadui maaskari?"

2 Kings 6:22

Elisha akajibu

Elisha alikuwa akimjibu Elisha mfalme wa Israeli swali.

Ungeweza kuwaua wale ambao uliokuwa umewachukua mateka kwa upanga na upinde wako?

Elisha anauliza hili swali lisilo na majibu kusisitiza kwa mfalme kwamba asiwaue hawa watu.

ulikuwa umechukuliwa mateka na upanga wako na upinde

Hii inawazungumzia maaskari wa mfalme kuwachukua watu mateka kana kwamba mfalme mwenyewe alikuwa ndiye aliye wateka. "maaskari wako walikamatwa mateka pamoja na panga zao na mikuki"

pamoja na upanga wako na upinde

Hizi ni silaha zilizokuwa zikitumika katika vita. "katika vita pamoja na upanga wako na upinde"

Weka mkate na maji mbele yao, kwamba wanaweza kula na kunywa

Hapa "mkate" unarejea kwa chakula kwa ujumla. "Kuwapatia chakula kula na maji kunywa,"

nenda kwa bwana wao

Hii inarejea kwa mfalme wa Shami.

Hivyo mfalme aliandaa chakula kwa ajili yao

Mfalme aliwaagiza watumishi wake kuandaa chakula. Hakuandaa chakula mwenyewe. "Kisha mfalme aliwaagiza watumishi wake kuandaa chakula kingi kwa ajili yao"

Hale makundi

"Hayo makundi"

halikurudi kwa mda mrefu katika nchi ya Israeli.

Hii inamaanisha kwamba hawakuishambulia Israeli kwa mda mrefu. "kuacha kuishambulia nchi ya Israeli kwa mda mrefu"

2 Kings 6:24

Ben Hadadi

Jina la mfalme wa Shami. Jina lake linamaanisha "mwana wa Hadadi."

kuiteka Samaria

Mfalme na jeshi lake waliiteka Samria. "waliiteka Samaria"

Tazama

Neno "tazama" hapa linatutahadharisha kuvuta usikivu kwenye habari za kushangaza zinazofuata.

kichwa cha punda kiliuzwa kwa

"gharama ya kichwa cha punda

vipande themanini vya fedha

"vipande 80 vya fedha"

sehemu ya nne ya kibaba

Hii inaweza kuandikwa katika vipimo vya kisasa. "sehemu ya nne ya lita" au " robo ya lita"

sehemu ya nne

"sehemu ya nne." Hii ni sehemu moja ya nne yenye sehemu sawa sawa.

kinyesi cha njiwa kwa

Neni linalokosekana linaweza kuongezwa. "kinyesi cha njiwa kiliuzwa kwa" au "ghara ya kinyesi cha njiwa"

akipita juu ya ukuta

"kutembea juu ya mji wa ukuta"

bwana wangu

Mwanamke anarejewa kwa mfalme kwa hili jina kumwonyesha heshima.

2 Kings 6:27

Alisema

"Mfalme wa Israeli alimjibu yule mwanamke,"

Kama Yahwe hawezi kukusaidia, nitakusaidiaje?

Mfalme anatumia hili swali lisilohitaji majibu kumwambia mwanamke kwamba hawezi kumsaidia. "Kama Yahwe hakusaidii, kisha siwezi kukusaidia."

je kuna kitu chochote kinakuja kutoka sehemu ya kupuria nafaka au shinikizoni

Mfalme anatumia hili swali lisilohitaji majibu kusisitiza kwamba hakuna chakula kinachopatikana.

Mfalme akaendelea

"Mfalme alisema." Hii inamaanisha kwamba waliendelea kuongea.

tulichemsha

"tulipika"

2 Kings 6:30

aliposikia yale maneno ya yule mwanamke

"msikilize mwanamke mwambie alikuwa na mwanamke mwingine alifanya,"

alirarua mavazi yake

Mfalme alichana mavazi yake ya nje kuonyesha huzuni yake. "alirarua mavazi yake katika huzuni"

sasa alikuwa akipita juu ya ukuta

alikuwa akitembea juu ya ukuta wa mji wakati mwanamke alipoitwa naye nje.

alikuwa amevaa nguo ya gunia chini, dhidi ya ngozi yake

Kwa kuvaa mavazi ya gunia hata kwa ajili ya vazi la ndani, mfalme alionyesha kwamba alikuwa na huzuni kubwa sana na kufadhaika sana.

Mungu afanye hivyo kwangu, na zaidi pia

Mfalme anasema anatumaini Mungu atamuadhibu na hata kuua kama Elisha nabii hatakufa kwa sababu ya mambo yaliyotokea katika mji wa Samaria. "Mungu aniadhibu na kuniua"

kama kichwa cha Elisha mwana wa Shefati

Hii inamrejea Elisha kufa, dhahiri kukatwa kichwa. "kama Elisha mwana wa Shafati hajakatwa kichwa leo"

2 Kings 6:32

Mfalme alimtuma mtu wa mbele yake

"Kuwa mbele ya mfalme" maana yake kuwa kuwa mmoja ya hawa watumishi wake. "Mfalme wa Israeli alimtuma mmoja wa watumishi wake kama mjumbe"

wakati mjumbe alipokuja kwa Elisha, aliwaambia wazee

Hapa Elisha anaongea na wazee mbele ya mjumbe wa mfalme alipofika. "wakati mjumbe alipokaribia kufika, Elisha akawaambia wazee"

"Ona jinsi huyu mwana wa muuaji alivytumwa kuchukua kichwa changu?

Elisha anatumia hili swali lisilohitaji majibu kuleta usikivu kwa wajumbe wa mfalme na kumdhalilisha mfalme.

mwana wa muuaje

Hii inamaanisha kwamba mfalme wa Israeli anatabia za mauaji. "huyu ambaye yuko kama muuaji" au "muuaji"

amemtuma

Maneno yanayokosekana yanaweza kuongezwa. "amemtuma mtu kwa"

kuchukua kichwa changu

Hii inamaanisha kumkata kichwa. "kukata kichwa changu"

Tazama

Elisha anatumia hili neno hapa kuleta usikivu wa wazee kwa kile anachotaka kukisema.

shika mlango funga juu yake

Kama mlango ukifungwa juu ya mtu inamaana kwamba umefungwa na kwamba hawawezi kuingia kupitia huo. "shika mlango funga ili asiweze kuingia"

Je sio sauti ya mguu wa bwana wake nyuma yake?

Elisha anatumia hili swali kuwahakikishia wazee kwamba mfalme anakuja sio mbali naye.

tazam, mjumbe

Neno "tazam" linatutahadharisha kufika kwa wageni

mjumbe akashuka chini kwenda kwake

Mjumbe, alifika, na mfalme alifanya, kama Elisha alivyokuwa amesema angefanya. Neno "alishuka chini kwake" linamaanisha kwamba walifika mahali ambapo alipokwa. "mjumbe na mfalme walifika"

Tazama, hii shinda

"Hakika, hii shida." "Neno "tazama" hapa inaongeza msisitizo kwa kile kifuatacho.

Kwa nini nimsubiri Yahwe tena?

Huyu mfalme anatumia hili swali lisilohitaji kijibiwa kusisitiza kwamba haamini kwamba Yahwe anaenda kuwasaidia.

2 Kings 7

2 Kings 7:1

kipimo cha unga mzuri kitauzwa kwa shekeli, na vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli

Inaeleza kwamba Waisraeli watakuwa wakilipa pesa kidogo kwa ajili ya hivi vitu kuliko walivyokuwa. Hii inaweza kuanza katika muundo tendaji. Watu watanunua kipimo cha unga mzuri kwa shekeli moja na vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli moja"

kipimo kimoja cha unga mzuri ... vipimo viwili vya shayiri

Hapa neno "kipimo" linatafsiri neno "sea," ambacho ni kipimo kikavu sawa na kama lita 7. "lita 7 za unga mzuri ... lita 14 za shayiri"

shekeli moja

Shekeli moja muunganiko wa uzito sawa na kama gram 11. "kama gram 11 za fedha" au Fedha moja ya sarafu"

nahodha ambaye mkono wake mfalme alijifunza

Cheo cha juu cha nahodha ambaye alikuwa msaidizi wa mfalme anazungumziwa kana kwamba mtu ambaye mfalme alijifunza mkono wake. "nahodha ambaye alikuwa karibu na mfalme" au "nahodha ambaye alikuwa msaidizi"

hata kama Yahwe angefanya madirisha mbinguni

Yahwe anafanya mvua kubwa kunyesha ili kufanya mimea kukua inazungumziwa kana kwamba Yahwe alikuwa akifungua madirisha mbinguni kupitia ambavyo amwagapo mvua chini. "hata kama Yahwe alisababisha mvua kubwa kunyesha kutoka mbinguni"

hili jambo linaweza kutokea?

Nahodha anauliza hili swali kueleza kutokuamini kwake. Hili swali lisilo na majibu linaweza kutafsiriwa kama kauli. "hii haitatokea!"

utaona ikitokea kwa macho yake mwenyewe

Neno "kwa macho yako mwenyewe" linasisitiza kwamba nahodha hakika ataona mambo ambavyo Elisha alivyovitabiri. "wewe mwenyewe utaona haya mambo yakitokea"

lakini hutakula chochote katika hicho

"lakini hutakula unga wowote au shayiri"

2 Kings 7:3

Sasa

Hili neno limetumika hapa kuvunja alama katika hadithi kuu. Hapa mwandishi anaanza kueleza mwanzo wa hadithi.

Kwa nini tuketi hapa hadi tutakapokufa?

I+ngawa hapa kulikuwa na watu wanne, ni kama mmoja wao aliuliza hili swali. Hili swali ni swali lisilo na majibu

Kama wakitupa uhai, tutakuwa hai, na kama wakituua, tutakufa tu

Wale watu wanne wenye ukoma wanasema kwamba Waaramu wangeweza kuwajaza ili kwamba waweze kuishi, au wanaweza kuwaua, ambapo hakutakuwa na ubaya zaidi wangekufa vyovyote.

2 Kings 7:5

wakati wa jioni

Hii inarejea mapema jioni baada ya jua kuzama, lakini kabla ya giza.

Washami kusikia sauti ya magari ya farasi, na sauti za farasi-sauti za jeshi jingine kubwa

Maaskari wa Shami walisikia s

jeshi la Washami kusikia sauti ya magari ya farasi, na sauti za farasi-sauti za jeshi jingine kubwa

Maaskari wa jeshi Washami walisikia sauti zilizokuwa zinalia kama jeshi kubwa linalokaribia kuwapiga. Hili halikuwa jeshi halisi, lakini Bwana aliwatengeneza kusikia hizi sauti.

waliambizana kila mmoja

"maaskari wa Washami waliambizana kila mmoja"

wafalme wa Wahitina Wamisri

Hapa neno "wafalme" linawakilisha majeshi ya haya mataifa. "majeshi ya Wahiti na Wamisri"

kuja juu yetu

"kutupiga sisi" au "kutushambulia"

2 Kings 7:7

Maelezo ya Jumla

Hivi ndivyo ilivyotokea baada ya Bwana kusababisha maaskari Washami kufikiri wamesikia jeshi kubwa la adui linakaribia kambi yao.

jioni

Hii inarejea jioni mapema baada ya jua kuzama, lakini nyuma yake ni giza.

nyara

Hii inarejea kwa vitu ambavyo huchukuliwa na jeshi lililoshinda kutoka jeshi jingine ambalo limeshindwa. Hapa inarejea kwa "fedha na dhahabu na nguo."

2 Kings 7:9

hadi macheo

"hadi asubuhi"

adhabu itatupata

Mmoja anawaadhibu watu wanne anazungumziwa kana kwamba adhabu ilikuwa mtu awakamataye. "watu watatuadhibu" au "mtu atatuadhibu"

waambie kaya ya mfalme

Hapa neno "kaya" inawakilisha watu ambao waishio katika nyumba ya mfalme. "mwambie mfalme na watu wake"

kama walivyokuwa

Habari za wazi inaweza kusambazwa katika tafsiri. "kama walivyokuwa wakati maaskari walipokuwa huko"

ndipo walipoambiwa ndani ya kaya ya mfalme

Hii inaweza kuanza katika muundo tendaji. "kisha watu waliiambia nyumba kaya ya mfalme"

2 Kings 7:12

walichotufanyia

"kinachopangwa kufanywa kwetu" au "walichofanya kutudanganya"

kuwakamata wakiwa hai

Hii inamaana kwamba wangewakamata watu na sio kuwaua.

farasi waliobaki, ambao waliobaki katika mji

Farasi wengi ni mali ya Waisraeli walikufa kwa sababu ya njaa. Maana ya hii inaweza kuwekwa wazi. "farasi katika mji ambao bado wako hai"

Wako kama mkutano wote wa Israeli waliobaki

Watu watakao enda kwa kambi ya Washamu watashiriki mauti ile ile kama mabaki ya Waisraeli waliobaki katika mji. Pengine watakufa kwa njaa, au labda kuwa kama karibu na Washami.

na tazama

Habari ya wazi inaweza kuongezwa kufanya maana wazi. "na tazama kama hawa wakoma walichokisema ni kweli?

2 Kings 7:14

Nenda na tazama

Habari ya uwazi inaweza kuongezwa kufanya maana wazi. "Nenda na tazama kama hawa wakoma walichikisema ni kweli"

Walifuatana nao kwenda Yordani

"Walifuata njia ya jeshi la Washamu kuchukua njia ya mto Yordani"

njia zote zilikuwa zimejaa nguo na vifaa

Hii inamaanisha kwamba watu waliviona hivi vitu vimetawanyika karibu na barabara walipokuwa wakisafiri. "kulikuwa na nguo na vitu vyote karibu na barabara"

2 Kings 7:16

wakaziteka nyara kambi

Hii inarejea kuchukua vitu kutoka jeshi lililoshindwa.

Hivyo kipimo cha unga mzuri uliuzwa kwa shekeli moja, na vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli moja

Hii inaweza kutafsiriwa katika muundo tendaji. "Hivyo watu waliuza kipimo kimoja cha unga mzuri kwa shekeli moja na vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli moja"

kipimo kimoja cha unga mzuri ... vipimo viwili vya shayiri

Hapa neno "kipimo" linatafsiri neno "sea," ambayo ni moja ya kipimo kikavu sawa na kama lita 7. "lita 7 za unga mzuri ... lita 14 za shayiri"

shekeli

Shekeli uzito mmoja sawa na kama gram 11. "kama gram 11 za fedha" au "fedha moja ya sarafu"

kama neno la Yahwe lilivyokuwa amesema

Hapa "neno" limuwakilisha Yahwe. "kama Yahwe alivyokuwa amesema"

nahodha ambaye mkono wake ulikuwa umejifunza

Nahodha wa daraja la juu aliyekuwa msaidizi wa mfalme anazungumziwa kana kwamba alikuwa mtu ambaye mfalme amejifunza mkono wake.

kumkanyaga chini

Kundi la watu lilikuwa katika kukurupuka kupata chakula katika kambi waligonga juu ya mtu na kumkanyaga hati kufa.

2 Kings 7:18

Maelezo ya Jumla:

Katika huu mstari, mwandishi amefupisha kilichotokea kwa kurudia matukio ambayo alielezea katika 7:1.

Mda kama huu

"Mda kama huu kesho"

vipimo viwili vya shayiri ... kipimo kimoja cha unga mzuri

Hapa neno "kipimo" unatafsri neno "sea," ambayo ni umoja wa kipimo kikavu sawa na lita 7. "lita 14 za shayiri ... lita 7 za unga mzuri"

shekeli

Shekeli ni moja ya uzito sawa na kama gram 11. "kama gram 11 za fedha" au "fedha moja ya sarafu"

Ona

"sana." Neno "Ona" hapa linaongeza msisitizo kwa kile kifuatacho.

hata kama Yahwe akiweka madirisha mbinguni

Yahwe analeta mvua kubwa sana kunyesha kwa ajili ya kufanya mimea ikue inazungumziwa kana kwamba Yahwe alikuwa akifungua madirisha mbinguni ambavyo ashuahapo mvua chini.

je hili jambo linaweza kutokea?

Nahodha anauliza hili swali kuelezea kutokuamini kwake. Hili swali linaweza kuatafsiriwa kama kauli.

utaona ikitokea kwa macho yako mwenyewe

Neno "kwa macho yako mwenyewe" linasisitiza kwamba nahodha anaona bila shaka mambo ambayo Elisha aliyoyatabiri.

lakini hutakula chochote katika hicho

"lakini hutakula chochote katika unga au shayiri"

2 Kings 8

2 Kings 8:1

Sasa

Hili neno linatumika hapa kugawanya mwanzoni mwa hadithi. Hapa mwandishi anaanza kueleza sehemu mpya ya hadithi.

yule mwanamke ambaye mwanaye alifufuliwa

Hadithi ya huyu mwanamke na mwanaye inapatikana kwenye 4:8.

alifufuliwa

"alisababisha akafufuliwa tena"

Inuka

"kuinika kutoka ulipo"

mtu wa Mungu

"Elisha, mtu wa Mungu"

2 Kings 8:3

kwa mfalme

Hii inarejelea kwa mfalme wa Israeli.

kwa ajili ya nyumba yake na nchi yake

wakati yule mwanamke alipokwenda, nyumba yake na vitu vyake vilizingirwa. Anaanza kuvirudisha kwa ajili yake.

Sasa

Hili neno linatumika hapa kugawanya kwenye hadithi kuu. Hapa mwandishi anatuambia historia kuhusu mfalme alichokuwa akifanya wakati mwanamke alipofika.

2 Kings 8:5

mtoto aliyekuwa amekufa alifufuliwa

"alisababisha mtoto aliyekuwa amekufa kuwa hai tena"

kwa ajili ya nyumba yake na nchi

Wakati yule mwanamke alipoondoka, nyumba yake na mali zake vilizingirwa. Anawaomba arudishwe.

kuhusu mwanaye

Hii inarejlea hadithi ya mwanaye akifa na Elisha kurejeshea uhai wake.

mafuno yote ya shambani mwake

Haya maelezo yanarejea kwa kiasi cha pesa ambacho mavuno ya shambani kwake yalikuwa ya thamani wakati alipokuwa mbali. Manufaa yote ya mavuno ya shamba lake"

2 Kings 8:7

Ben Hadadi

Hili ni jina la mfalme wa Shami. Jina lake linamaanisha "mwana wa Hadadi."

Hazaeli

Hili ni jina la kiume.

Chukua zawadi

Hazaeli alichukua zawadi nyingi, sio moja tu. "chukua zawadi nyingi"

katika mkono wako

Hili neno "katika mkono wako" ni lugha inayomaanisha kwake kuchukua zawadi pamoja naye. "pamoja nawe"

mtu wa Mungu

Elisha, mtu wa Mungu"

kushauriana na Yahwe kupitia yeye, kusema

"muulize Elisha kumwambia Yahwe"

kubeba ngamia arobaini

Hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji. "alibeba ngamia arobaini"

ngamia arobaini

"ngamia 40"

Mtoto wako Ben Hadadi mfalme wa Shamii

Ben Hadadi hasa alikuwa mwana wa Elisha, lakini Hazaeli alimuita ili kwamba kuonyesha uhusiano wa karibu kati yao. "Ben Hadadi mfalme wa Shami, ambaye ni kama mtoto kwako,"

2 Kings 8:10

hadi alipoona aibu

"hadi Hazaeli alijisikia hana raha"

bwana wangu

Hazaeli anarejea kwa Elisha kwa njia hii kumheshimu yeye.

Kwa najua

Mungu alimuonyesha Elisha nini kitchukua nafasi mbeleni.

utafanya

Neno "wewe" linamrejea Hazaeli na kumrejea yeye mwenyewe na maaskari chini ya utawala wake wakti wakiwa mfalme. "utasababisha itokee" au "utawaagiza maaskari wako"

Utaweka ... utawaua

Neno "wewe" linamuwakilisha Hazaeli hapa kurejea kwa maaskari na sio kwa Hazaeli mwenyewe. "Ninyi maaskari mtawekwa ... maaskari wako watauawa"

kuwaseta vipande vipande watoto wao

"kuwaponda watoto wao wadogo. "Haya ni maelezo ya ukatili ya maaskari kuwau watoto.

kuwaua watoto wao wadogo kwa upanga

Hii inamaanisha kwamba wanaume watauawa kwa kwenye vita. Upanga ulikuwa silaha kubwa iliyokuwa ikitumika katika vita. "kuwaua watoto wao wa kiume wadogo katika vita"

kupasua mimba zao wanawake

Hii inarejea hasa kupasua wazi matumbo yao. "pasua wazi matumbo ya mimba za wanawake kwa upanga"

2 Kings 8:13

Mtumwa wako ni nani, ambaye atafanya hili jambo hili kubwa

Hazaeli anarejea kwake mwenyewe hapa kama mtumishi wa Elisha. Hazaeli anatumia hili swali lisilodai jibu kusisitiza kwamba hafikirii angefanya mambo mabaya ambayo Elisha ameyasema.

jambo hili kubwa

"jambo hili kubwa." Hapa neno "kubwa" linarejea kwa kitu ambacho kina madhara makubwa na kibaya.

Yeye ni mbwa tu

Hazaeli anajizungumzia mwenyewe. Anaongea kwa hali ya chini na kupungukiwa na ushawishi kwa kujilinganisha na mbwa. Hapa mbwa anawakilisha mbwa mnyama wa chini.

kuja kwa bwana wake

Neno "bwana wake" inamrejea Ben Hadadi.

uso hivyo basi akafa

Hii inamaanisha kwamba Ben Hadadi akakosa hewa kwenye blangeti. Maana kamili ya hii sentensi inaweza kuwekwa wazi. "uso. Ben Hadadi hakuweza kupumua kupitia hiyo, na hivyo akafa"

2 Kings 8:16

Maelezo ya Jumla:

Yohoramu akawa mfalme wa Yuda.

Katika mwaka wa tano wa Yoramu mwana wa Ahabu, mfalme wa Israeli

Hii inaeleza kipindi ambacho Yehoramu alipoanza kutawala kueleza mda gani Yoramu, mfalme aliyepo wa Israeli, alitawala. "Katika tano ambao Yoramu mwana wa Ahabu alipokuwa mfalme wa Israeli"

mwaka wa tano

"mwaka wa 5"

Yoramu alianza kutawala

Yoramu, mwana wa Yehoshafati, akawa mfalme wa Yuda.

umri wa miaka kumi na mbili

umri wa miaka miwili - "miaka 32"

2 Kings 8:18

Yehoramu akaenenda katika njia za wafalme wa Israeli

Hapa "kuenenda" ni lugha inayorejea jinsi alivyoishi na kutawala kama mfalme. Katika kipindi hiki kihistoria, wafalme wa Israeli walikuwa wafalme waovu. Maana halisi ya hii sentensi inaweza kuwekwa wazi. "Yehoramu alikuwa mfalme muovu, kama wafalme wengine wa Israeli waliotawala kabla yake alivotawala"

kama nyumba ya Ahabu ilivokuwa ikifanya

Hapa "nyumba" ya Ahabu inarejea kwa wadau wa familia ya Ahabu na uzao wake mpya. Ahabu ni mkwe wa Yoramu. "sawa kama familia iliyobaki ya Ahabu ilivyokuwa inafanya"

kwa kuwa alikuwa na binti wa Ahabu kama mkewe

Yehoramu alimuoa binti Ahabu.

alifanya yaliyo maovu usoni mwa Yahwe

Hapa "uso" wa Yahwe unarejea kwa yale ayafikiriyo. "alifanya mambo ambayo Yahwe aliyoyasema yalikuwa maovu"

angamiza Yuda

Hapa "Yuda" ni kielelezo kwa ajili ya watu walioishi huko. "angamiza watu wa Yuda"

tangu alipomwambia kwamba atampatia wazao

"tangu Yahwe alipomwambia Daudi kwamba angeupatia uzao wa Daudi." Hii inarejea kwa ahadi ya Yahwe kwa Daudi kwamba ukoo wake ungeitawala Yuda. Maana kamili ya hii sentence inaweza kuwekwa wazi. "tangu alipomwambia Daudi kwamba huu ni ukoo utakaoitawala Yuda.

2 Kings 8:20

Edomu akaasi kutoka chini

"Edemu aliasi juu ya"

mkono wa Yuda

Hapa neno neno "mkono" inarejea kwa utawala wa Yuda, na "Yuda"

wakamuweka mfalme juu yao

"kamteua mfalme kutawala juu yao"

Kisha Yehoramu akavuka

ilikuwa kuvuka nini "akavuka" inaweza kuelezwa wazi. "Kisha Yehoramu akavuka mistari ya adui"

Ikatokea akainuka usiku

"Kisha, usiku, akainuka"

akainuka

Hapa neno "yeye" inawakilisha Yehoramu na kurejelea kwa yeye mwenyewe na makamanda wake. "yeye na makamanda wake"

2 Kings 8:22

Maelezo ya Jumla:

Mfalme Yoramu wa Yuda akafa na mwana wake Ahazia akawa mfalme.

Edomu aliasi dhidi ya utawala wa Yuda katika siku hizi

"Hivyo baada ya hayo, Edomu hakutawaliwa tena na Yuda, na bado iko hivyo" (UDB)

utawala wa Yuda

Hapa "Yuda" inarejea kwa mfalme wa Yuda. "utawala wa mfalme wa Yuda" au "mamlaka ya mfalme wa Yuda"

hadi sasa

hadi hiki kitabu kilipoandikwa

Libna aliasi pia mda huo huo

Libna aliasi juu ya mfalme wa Yuda kama Edomu alivyokuwa. "Katika kipindi hicho hicho, Libna pia aliasi juu ya mfalme wa Yuda"

Libna

Hili ni jiji jingine ambalo lililokuwa sehemu ya Yuda kwa asili. Hapa "Libna" inarejea kwa watu wanaishi hapa. "watu wa Libna"

Kama kwa mambo mengine yanayomhusu Yoramu, yote aliyoyafanya

"Kusoma zaidi kuhusu hadithi ya Yoramu na kile alichokifanya,"

je hayajaandikwa ... Yuda?

Hili swali linatumika pengine kujulisha au kuwakumbusha wasomaji kwamba habari kuhusu Yoramu ipo katika hiki kitabu. "haya mambo yameandikwa ... Yuda." au "unaweza kusoma kuhusu wao ... Yuda."

Yoramu alikufa na kupumzika na baba yake, na alizikwa na baba yake

Hapa "kupumzika" ni heshima ya kurejea kwa mtu kufa. Baada ya kufa, mwili wake ulizikwa sehemu moja na miili ya baba zake. Neno "alizikwa" linweza kuelezwa katika muundo tendaji. "Yoramu alikufa, na walimzika pamoja na baba zake"

Kisha Ahazia mwanaye akawa mfalme

"Kisha Ahazia, mwana wa Yoramu, akawa mfalme baada ya yeye kufa"

2 Kings 8:25

Maelezo ya Jumla:

Ahazia akawa mfalme wa Yuda.

Katika mwaka wa kumi na mbili wa Yuoramu mwana wa Ahabu, mfalme wa Israeli

Hii inaeleza mda ambao Ahazi alianza kutawala kama mfalme wa Yuda kwa kusema ni mda gani Yoramu, mfalme wa sasa wa Israeli, alitawala, "katika mwaka wa kumi na mbili ambao Yoramu mwana wa Ahabu alikuwa mfalme wa Israeli"

mwaka wa kumi na mbili

"mwaka wa 12"

miaka ishirini na mbili

ishirini na mbili - miaka 22"

Athalia ... Omri

Athalia ni jina la mwanamke. Omri ni jina la mwanamume.

Ahazia alienenda katika njia za

Hapa "enenda" inarejea tabia yake au vile alivyoishi. "Ahazia aliishi kama wengine"

nyumba ya Ahabu

Hapa "nyumba" ya Ahabu inarejea kwa familia yake. "familia ya Ahabu"

alifanya yaliyo maovu usoni mwa Yahwe

Hapa "uso" wa Yahwe unawakilisha kile afikiriacho. "alifanya mambo ambayo Yahwe aliyahesabu kuwa maovo" au "alifanya mambo ambayo Yahwe alisema yalikuwa maovu"

mkwewe kwenye nyumba ya Ahabu

mkwewe kwenye nyumba ya Ahabu* - Hii inaielezea mahusiano ya familia ya Ahazia kwa Ahabu. Baba yake na alimuoa binti wa Ahabu. Maana ya hii inaweza kuwekwa wazi. "mwana wa mkwewe na Ahabu" au "mjukuu wa Mfalme wa Ahabu"

2 Kings 8:28

Ahazia akaenda pamoja na Yoramu mwana wa Ahabu, kupigana dhidi ya Hazaeli, mfalme wa Shamu

Majina ya wafalme watatu wametajwa hapa ni maneno yenye maana sawa na pia yanareje kwa adui zao ambao walioongozana nao. Jeshi la Ahazia lilijiunga na jeshi la Mfalme Yoramu wa Israeli kupigana juu ya jeshi la Mfalme Hazaeli wa Shami" (UDB)

kuponywa

Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji. au "kupona"

juu ya Hazaeli mfalme wa Shami

Hapa "Hazaeli" inamrejea mwenyewe na jeshi lake. "jeshi la Hazaeli mfalme wa Shami"

Yoramu alijeruhuiwa

Hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji. "Washami walimjeruhi Yoramu"

2 Kings 9

2 Kings 9:1

wana wa manabii

Hii haimaanishi kwamba walikuwa wana wa manabii, badala yake, walikuwa kundi la manabii.

katika mkono wako

Neno "katika mkono wako" ni lugha inayomaanisha kwake yeye kushika chupa pamoja naye. "pamoja nawe"

Ramothi Geliadi

Hili ni jina la kiume.

Yehu mwana wa Yehoshafati mwana wa Nimshi

Hii inamaanisha kwamba Yehoshafati ni baba yake na Yehu na kwamba Nimshi ni baba yake Yehoshafati.

marafiki

Hawa ni watu ambao Yehu aliokuwa ameketi nao.

kumpeleka

"kwenda pamoja naye kwa"

chumba cha ndani

"chumba binafsi"

2 Kings 9:4

tazama

Mwandisha anatumia neno "tazama" kupeleka umakini kwa kile kifuatacho.

manahodha wa jeshi walikuwa wameketi

Yehu alikuwa ameketi miongoni mwa manahodha. "Yehu na baadhi maafisa wa majeshi mengine waliokuwa wameketi pamoja"

Yupi kati yetu

Neno "sisi" linarejea kwa Yehu na manahodha wengine.

2 Kings 9:7

Maelezo ya Jumla:

Nabii mdogo anaendelea kunena na Yehu, ambaye alikuwa amepakwa mafuta kama mfalme juu ya Israeli.

niweze kulipiza kisasi cha damu ya watumishi wangu manabii, na damu ya watumishi wote wa Yahwe

Hapa manabii na watumishi "damu" linarejea kwa vifo vyao. "naweza kulipa kisasi cha kifo cha watumishi wangu manabii na watumishi wote wa Yahwe" au "hivyo basi ninaweza kuwaadhibu kwa kuwaua watumishi wangu manabii na watumishi wote wa Yahwe"

na damu

Neno linalokosekana "kulipa kisasi" linaweza kuongezwa "na kulipa kisasi cha damu"

nani aliuawa kwa mkono wa Yezebeli

"ambaye Yezebeli aliwaamuru watumishi wake kuua"

kwa mkono wa Yezebe

Hii inamaanisha kwamba Yezebeli aliwaamuru watu kuuawa. "kwa agizo kutoka Yezebeli" au "kwa amri ya Yezebeli"

Kwa kuwa nyumba yote ya Ahabu itaangamia, na nitamkatilia mbali kila mtoto wa kiume wa Ahabu

Hapa ku "kata" maana yake kuuawa. "Kwa ajili ya familia yote ya Ahabu itaangamia, na nitamfanya kila mtoto wa kiume katika familia yake kuuawa" au "Kila mwanajumuiya wa familia ya Ahabu atakufa, pamoja kila mtoto wa kiume"

kila mtoto wa kiume

Hili neno limetumika kumrejea kila mwanamume, lakini imwekwa bayana "mtoto

2 Kings 9:9

Maelezo ya Jumla:

Nabii mdogo anaendelea kunena maneno ya Yahwe kwa Yehu, ambaye alikuwa amepakwa mafuta kama mfalme juu ya Israeli.

Nitaifanya nyumba ya Ahabu kama

Hii inamaanisha kwamba Mungu atamwangamiza Ahabu na familia yake kama alivyomwangamiza Yeroboamu na Baasha na familia zao. "nitaiendesha nyumba ya Ahabu kama ninavyoiendesha ya"

nyumba ya

Hili neno limetumika katika huu mstari mara tatu. Kila wakati, neno "nyumba" linarejea kwa "familia" ya mtu maalumu. "familia ya"

Nebati ... Ahiya

Haya ni majina ya wanaume.

Mbwa watamla Yezebeli

Hii inamaanisha kwamba mbwa wataila maiti yake. "Mbwa wataila maiti ya Yezebeli"

2 Kings 9:11

watumishi wa bwana wake

Hii inarejea kwa maafisa wengine waliokuwa wakimtumikia Mfalme Ahabu.

mwenda wazimu

"mtu mjinga"

Unamjua huyo mtu na mambo asemayo

Yehu asema kwamba yeye ni nabii mdogo na wote ni familia pamoja na aina ya mambo yote ya jumla yasemwayo na manabii.

Tuambie

"Tuambie alichokwambia"

Amesema hivi na vile juu yangu

"Alinena kuhusu baadhi ya mambo"

kila mmoja wao akachukua vazi haraka na kuweka chini ya Yehu

Katika utamaduni hii, kuweka nguo juu ya ardhi ilikuwa njia ya kumheshimu mfalme, ili kwamba miguu yake isiguse ardhi kavu.

Wakapiga baragumu na kusema

Sio kila mmoja alipiga baragumu. Inaelekea mtu mmoja alipiga tarumbeta. "mmoja wao walipiga tarumbeta na wote walisema"

2 Kings 9:14

Nimshi

Nimshi ni jina la baba wa Yehoshafati

Basi Yoramu

Hili neno limetumika hapa kuvunja alama katika hadithi kuu. Hapa mwandishi anaeleza habari ya historia jinsi Yoramu alivyokuwa amejeruhiwa na kwenda kupona katika Yezreeli.

Israeli yote

Hii inarejea kwa jeshi la Waisraeli pekee na sio kwa kila mmoja aishie katika Israeli. "yeye na jeshi lake" au "yeye na jeshi la Israeli"

kuponywa

"kupona kutokana na"

majeraha aliyokuwa ameyapewa na Washami

Hii inamaanisha kwamba alikuwa amejeruhiwa katika vita pamoja na Washami. "majeraha ambayo Yoramu aliyapata kipindi cha vita pamoja na jeshi la Shami"

juu ya Hezekia mfalme wa Shamu

Hii inamrejea Hazaeli na jeshi lake. "juu ya na jeshi lake"

Hazaeli

Hazaeli alikuwa mfalme wa Shami

Yehu aliwaambia watumishi wa Yoramu

Hii inawarejea maafisa waliokuwa pamoja na Romath Gileadi.

Kama hili ni wazo lako

"Kama upo kwenye makubaliano pamoja nami" Yehu anatumia hili neno kurejea kama watu wanamuunga mkono kuwa mfalme na maamuzi yake. "Kama kweli mnataka niwe mfalme wenu"

ili kwenda kusema hizi habari katika Yezreeli

Hii inarejea kumwambia Yoramu na jeshi lake la mbinu za Yehu. "kumuonya mfalme Yoramu na jeshi lake katika Yezreeli"

Basi Ahazia

Neno "basi" limetumika hapa kuvunja alama katika kichwa cha hadithi. Hapa mwandishi anaeleza habari za nyumba kuhusu Ahazia kumtembelea Yoramu.

2 Kings 9:17

mlinzi

"ulinzi"

lile kundi la Yehu alipokuwa akija kwa mbali kidogo

"Yehu na watu wake walipokuwa bado wako mbali"

Unataka kufanya nini na amani?

Yehu anatumia swali lisilohitaji jibu kumwambia mjumbe kwamba haimuhusu kama akija katika amani au hapana.

Mjumbe amekutana nao, lakini harudi

Mlinzi alimwambia Mfalme Yoramu kwamba yule mtu aliyemtuma harudi pamoja majibu ya swali la mfalme.

2 Kings 9:19

Kisha akapeleka mpanda farasi wa pili, ambaye alikuja kwao

"Kisha mfalme Yoramu akamtuma mjumbe kuendesha farasi, ambaye alitoka nje kumlaki Yehu na jeshi lake"

mtu wa pili

"mtu wa 2"

Wewe una nini na amani

Yehu anatumia hili swali lisilohitaji majibu kumwambia mjumbe kwamba haimuhusu kama akija kwa amani au hapana. Hii inaweza kuandikwa kama sentensi. ""Haiko juu yako kujua kama nimekuja kwa amani!"

Kwa kuwa hilo gari la farasi limekuwa likiendeshwa ndivyo ambavyo Yehu mwana wa Nimshi aendeshavyo

"Kwa sababu dereva wa gari la farasi huendesha kama ambavyo yehu mwana wa Namshi huendesha"

2 Kings 9:21

kila mmoja kwenye gari lake la farasi

"kila mmoja katika gari lake mwenyewe la farasi" (UDB)

kila mmoja kwenye

"Walipomfikia Yehu, alikuwa kwenye"

Nabothi

Hili ni jina la mwanamume.

Myezreeli

Hii inarejea kwa mtu kutoka Yezreeli.

Amani gani hapo, wakati uzinzi wa ukahaba hufanywa na uchawi wa mama yako Yezebeli umejaa tele?

Yehu anatumia hili swali lisilohitaji majibu kueleza kwa nini haji kwa amani.

2 Kings 9:23

akarudisha magari yake ya farasi na kukimbia

"akageuza gari lake la farasi kuzunguka kujaribu kukimbia"

udanganyifu

udanganyifu au hila

kwa nguvu zake zote

"kwa nguvu zake zote" au "kwa uwezo wake wote"

akaanguka chini kwenye gari lake la farasi

Yoramu akafa kwa kupigwa na mshale. "Yoramu akaanguka chini akafa katika gari lake la farasi"

2 Kings 9:25

Bidkari

Hili ni jina la mwanamume.

Mchukue na mtupie

"Ichukue maiti yake na itupe"

Fikiri kuhusu ambavyo

"Kumbuka"

baada ya Ahabu baba yake

Hii inamaanisha kwamba waliendesha katika gari la farasi nyuma ya gari la farasi la Ahabu. "nyuma ya baba yake gari la farasi la Ahabu"

Yahwe akamuweka huyu nabii dhidi yake

"Yahwe alinena huu unabii huu dhidi ya Ahabu"

damu ya Nabothi na damu ya watot wake

Hapa neno "damu" linarejea kwa "kuua" "mauaji ya Nabothi na mauaji ya watoto wake"

nitakulipa

Hii inamaanisha kwamba atamuadhibu Ahabu kama astahilivyo kwa ajili ya uovu alioufanya. "nitakupatia unachostahili kwa ajili ya uovu ulioufanya"

mchukue na mtupie kwenye hiyo sehemu, hilo shamba

"ichukue maiti ya Yoramu na itupe kwenye shamba lile lile, shamba la Nabothi"

kuleta kupita kile tulichokuwa tumeambiwa kingetokea

"kutimiza unabii ulionenwa kwetu"

tuliambiwa itatokea kwa neno la Yahwe

"kile Yahwe alichosema kingetokea" (UDB)

2 Kings 9:27

Maelezo ya Jumla:

Hii ni hesabu ya kile kilichotokea kwa Ahazia, mfalme wa Yuda, baada ya Yehu kuua Yoramu.

alipoliona hili

"alipoona kilichotokea kwa Yoramu"

Bethi Hagani ... Guri ... Ebleamu ... Magido

Haya ni majina ya mahali

mahali pa kupandia Guri

Neno "kupandia" linamaanisha walikuwa wakipanda juu ya kilima wakiwa wanasafiri juu ya barabara ya Guri. "juu ya barabara ya kupanda juu kwenda Guri"

baba zake

"babu zake"

2 Kings 9:29

katika mwaka wa kumi na moja wa Yoramu mwana wa Ahabu

Hii inaeleza wakati ambao Ahazia alianza kutawala kwa kuanza wakati gani mfalme aliyepo wa israeli alikuwa ametawala. "katika mwaka wa kumi na moja wa ambao Yoramu mwana wa Ahabu alipokuwa mfalme wa Israeli"

mwaka wa kumi na moja

"mwaka wa 11"

2 Kings 9:30

akapaka wanja macho yake, akatengeneza nywele zake vizuri

"kuweka mwonekano, alifanya nyele zake kuonekana nadhifu"

Unakuja kwa amani, wewe Zimri, bwana wako muuaji?

Yezebeli anatumia hili swali lisilo na majibu kumshtaki Yehu kwa kutokuja kwa amani. "Yamkini unakuja bila amani, wewe Zimri, bwana wako muuaji!"

wewe Zimri, bwana wako muuaji

Hapa Yezebeli anamuita Yehu "Zimri" kusema kwamba yeye ni muuaji. Zimri alikuwa kamanda wa jeshi la Israeli lililomuua mfalme wa Israeli kwa sababu alitaka kuwa mfalme. "umemuua bwana wako, kama Zimri alivyomuua bwana wake"

Zimri

Hili ni jina la mwanamume.

Ambaye yu upande yangu

"Kuwa juu ya upande wa mtu mwingine" maana yake kuwa mwaminifu kwao na kuwasaidia. "Ambaye aliye mtiifu kwangu"

2 Kings 9:33

Kumtupa chini

Yehu alimwambia towashi kumtupa Yezebeli nje ya dirisha.

Hivyo wakamtupa Yezebeli chini

Matowashi wakamtupa Yezebeli nje ya dirisha la juu akafa wakati alipopiga chini.

na Yehu akamseta chini ya miguu

Hii inamaanisha kwamba aliende farasi wake ambao walikuwa wakivuta gari lake kuseta mwili wake chini ya miguu yake"

Mtazameni

Neno "mtazameni" maana yake kutoa umakini kwa yeyote aliyewekwa wazi. "Sasa nenda kwa"

kwa kuwa ni binti wa mfalme

kwa kuwa Yezebeli alikuwa binti wa mfalme, ilikuwa lazima kumzika nabii wake. "kwa sababu alikuwa binti wa mfalme na kwa hiyo angezikwa inavyostahili" (UDB)

2 Kings 9:35

hawakumkuta ila

"hawakumkuta ila mwili wake"

viganja vya mkono wake

Kiganja ni sehemu ya ndani ya mkono.

Mtishibi

Hii inarejea kwa mtu kutoka mji wa Tishbi.

mwili wa Yezebeli utakuwa kama kinyesi juu ya uso wa mashamba katika nchi ya Yezreeli, kwa hiyo basi hakuna atakayeweza kusema

Hii inazungumzia vipande vya mwili wa Yezebeli kutawasambaa katika shamba kana kwamba walikuwa kinyesi kilichosambazwa katika shamba. Tangu vipande vya mwili wake vilipokuwa vidogo na kutawanyika hapakuwa na kitu ambacho kingeweza kukusanywa na kuzikwa. "vipande vya mwili wa Yezebeli utatawanyika kama kinyesi katika mashamba, ili kwamba pasiwe na mtu atakayeweza kuitambua na kusema"

kinyesi

"mbolea" Hii inarejea dhaihiri kwenye kwa kinyesi kilichotumika kama mbolea.

basi hakuna atakayeweza kusema, "Huyu ni Yezebeli."

"basi hakuna atakayeweza kueleza huyu alikuwa Yezebeli."

2 Kings 10

2 Kings 10:1

zao sabini

"zao 70"

Yehu aliandika barua na kuwatuma kwenda Samaria

Hii inamaanisha kwamba Yehu alituma mjumbe kupeleka barua. "Yehu aliandika barua na kumtuma mjumbe kuzipeleka Samaria"

kusema, "Wa bwana wako

"Barua zilisema, 'Ya bwana wako"

kumuweka juu ya kiti cha kifalme cha baba yake

Hapa, kumuweka juu ya kiti cha kifalme inamaanisha kuteuliwa kama mfalme. "kumfanya mfalme katika mahali pa baba yake"

kwa ajili ya safu ya ufalme wa bwana wako

"uzao wa bwana wako" Hapa huyo mtu ambaye waliye mchagua kuwa mfalme anarejewa kwa safu ya uzao ufalme wa Ahabu. "kulinda uzao wa bwana wako" au "kumlinda"

2 Kings 10:4

Lakini waliogopa

"Kisha waliogopa"

wafalme wawili

"wafalme wawili, Yoramu na Ahazia"

wasingeweza kusismama mbele ya Yehu

Hapa "simama" inamaanisha kuweza kustahimili chini ya shida. "wasingeweza kustahimili juu ya Yehu" au "wasingeweza kumpinga Yehu"

Hivyo tunawezaje kusimama?

Uzao unatumia swali lisilohitaji jibu kuonyesha kwamba hawawezi kusimama juu ya Yehu. "Hatuwezi kusimama juu yake popote!" au "Hatuwezi kumpinga popote!"

huyo mtu aliyekuwa juu ya mji

"meya wa mji" (UDB). Hapa kuwa "mwisho" kitu inamaanisha kuwa na mamlaka na wajibu juu yake. "yule mtu aliyekuwa msimamizi wa mji"

wale waliowalea watoto

Hii inarejea kwa watu waliowalea watoto wa mfalme. "wale waliowalea watoto wa mfalme"

Fanya kilicho chema katika macho yako

Hapa "mcho" ya Yehu inarejea kwa "uso" wake. "Uso" wake inarejea kwa kile afikiriacho. "Fanya kilicho chema katika uso wako" au "Fanya chochote ufikiriacho ni bora"

2 Kings 10:6

mara ya pili

"mara ya 2"

upande wangu

Kuwa "upande wa mwingine" inamaanisha kuwa mttifu kwao na kuwasaidia. "mwaminifu kwangu"

sikia

kusikiliza na kutii

sauti yangu

Hapa "sauti" ya Yehu inarejea kile akisemacho. "kwa kile asemacho"

mtachukua vichwa ... na mje kwangu

Inaonyesha kwamba wanatakiwa kuleta vichwa vya uzao wa Ahabu na kuviweka kwa Yehu. "mtachukua vichwa ... na kuvileta kwangu"

mtachukua vichwa ... na mje kwangu

Inaonyesha kwamba wanatakiwa kuleta vichwa kwa uzao wa Ahabu na kuviweka kwa Yehu. "mtavichukua vichwa ... na kuvileta kwangu"

mtachukua vichwa vya watu wa uzao wa bwana wenu

Hii inarejea kuwaua na kuwaondoa vichwa vyao. "kuua uzao wa bwana wenu na kuvikata vichwa vyao"

sabini katika namba ... watu sabini

"70 katika namba ... watu 70"

waliokuwa wakiwapandisha juu

Hii inamaanisha kwamba walikuwa wakiwasimamia na kuwafundisha. "waliokuwa wakiwalea" au "waliokuwa wakiwasimamia"

na kuwapeleka kwa Yehu

Hii inaanisha kwamba waliwatuma watu kupeleka vikapu kwa Yehu. "na kuwapeleka watu kuwachukua kwa Yehu"

2 Kings 10:8

wa wana wa mfalme

"wa ukoo wa Ahabu" (UDB)

Yehu alitoka na kusimama

"Yehu alienda kwenye lango la mji na kusimama mbele ya watu"

huna hatia

Inaweza kuelezwa wazi walikuwa hawana hatia kwa lipi. "Huna hatia kwa kile kilichotokea kwa Yoramu na familia yake" au "Huna hatia kwa hili jambo"

Ona

Yehu anatumia hili neno hapa kuleta usikivu wa watu kwa kile anachotaka kukisema"

lakini ni nani aliyewaua hawa wote?

Yehu anatumika swali lisilo hitaji majibu kuwafanya watu kufikiria kwa undani kuhusu hii hali. Hii inaweza kuandikwa kama sentensi. "lakini ilikuwa mapenzi ya Yahwe hawa watu kufa"

2 Kings 10:10

hakika tafakarini

"elewa" au "kuwa makini usipingika kwamba"

hakuna sehemu ya neno la Yahwe ... litaanguka kwenye nchi

Hii inazungumzia kila kitu kinachotokea kwamba Yahwe amesema kitatokea kana kwamba kilikuwa kitu ambacho kilikuwa kimekufa na kuanguka katika nchi.

Yahwe amefanya

Hii inamzungumzika Yahwe kuufanya uzao wa Ahabu kuuawa kana kwamba amewaua yeye. "Yahwe amefanya itokee"

Hivyo Yehu aliwaua wote ... na makuhani wake

Yehu hakuwaua hawa watu wote mwenyewe, isipokuwa aliwaamuru wauawe. "Hivyo Yehu aliwaamuru wote ... kuuwa"

wote waliosalia

"wote waliokuwa hai" au "wote waliokuwa wameondoka"

hakuna hata mmoja wao alisalia

hii inamaanisha kwamba wote wote waliuawa. au "hadi wote walipokufa"

2 Kings 10:12

Bethi Ekedi ya mchungaji

hili lilikuwa jina la mahali ambapo kondoo walipokuwa wakinyolewa.

kwenda chini kusalimia

"kwenda kutembelea"

watoto wa mfalme

"watoto wa Mfalme Yoramu"

Kuwachukua hai

Hii inamaanisha kuwakamata, lakini sio kuwaua. "Kuwatwaa!" (UDB) au "Kuwakamata!"

Hivyo waliwachukua wakiwa hai

"Hivyo waliwakamata"

watu arobaini na mbili

watu wawili "watu 42"

Hakumwacha hata mmoja wao akiwa hai

Hii inaweza kuelezwa katika muundo hasi. "aliwaua wote"

2 Kings 10:15

Yonadabu mwana wa Rekabu

Hili ni jina la mwanamume.

Je moyo wako uko na mimi, kama moyo wangu ulivyo pamoja na wako? ... "ndiyo."

Hapa "moyo" wa mtu inarejea kwa uaminifu wao. Kama uaminifu wa mtu uko "pamoja na mtu," inamaanisha kwamba ni waaminifu kwa hao watu. "utakuwa mwaminifu kwangu, kama nitakavokuwa mwaminifu kwako? ... 'ndio."'

Kama ipo, nipatie mkono wako

"Kama ni hivyo weka mkono wako ndani yangu" au "Kama ni hivyo, tushikane mikono" Katika tamaduni nyingi, wakati watu wawili washikanapo mokono, inaimarisha makubaliano yao.

na uone wivu wangu

Neno "wivu" unaweza kuelezwa kama kivumishi. "na tazama jinsi nilivyo na wivu"

safu ya familika ya kifalme

"familika yote ya kifalme"

kama walivyokuwa wameambiwa kabla ya neno la Yahwe, ambalo aliloambiwa Eliya

"kukamilisha unabii ambao Eliya alikuwa ameunena, ambao yahwe aliwapatia"

2 Kings 10:18

akawakusanya

"akawaita"

watu wote pamoja

"watu wote wa Samaria"

kumwokoa zaidi

"kumwokoa zaidi kuliko Ahahbu"

Asikosekane mtu hata mmoja

"Usimwache mtu hata mmoja nje"

Yeyote ambaye hatakuja hataishi

Hii inamaanisha kwamba kama hawatakuja watapingwa. "Tutawapinga yeyote ambaye hatakuja"

Tengeni mda

Hii inamaanisha kuonyesha na kuandaa majira ya mda kwa ajili ya kitu. Katika kesi hii walitakiwa kuandaa kwa ajili ya mkutano wa Baali. "Andaa"

2 Kings 10:21

Kisha Yehu akaituma

Hii inamaanisha kwamba kutuma wajumbe kuuchukua huu ujumbe kupitia nchi. "Kisha Yehu akawatuma wajumbe" au "Kisha Yehu akatuma ujumbe"

hivyo basi hakuna mtu hata mmoja ambaye aliacha kuja

"hivyo basi kila mwabudu Baali alikuwa huko" au "hivyo basi kila mtu akaja"

lilijaa

"waliijaza"

aliyekuwa anatunza kabati la nguo za makuhani

Hapa "kutunza" kitu inamaanisha kuiangalia na kuisimamia. "ambaye alikuwa msimamizi wa kabati la mfalme"

2 Kings 10:23

akawaambia wamwabuduo Baali

"na Yehu akawaambia watu waliokuwa katika hekalu kumwabudu Baali"

lakini wamwabuduo Baali pekee

"lakini wale wanaomwabudu Baali wako hapa"

Kama mtu yeyote miongoni mwa hawa watu ambao nimewaleta kwenye mikono yenu atoroke

Hapa "mikono" ya watu inarejea kwa "utawala" wao. Kwa kuwa katika lindo kuzunguka hekalu walikuwa katika utawala wa lindo na ilikuwa juu yao eidha watu waliweza kutoroka au hapana. "Kama mmoja wa hawa watu niliowaleta katika utawala wako wakitoroka" au "Kama yeyote katika hawa watu walio ndani wakitoka"

yeyote atakayemwacha huyo mtu atoroke, maisha yake yatachukuliwa kwa ajili ya yule aliyeokoka

"tutamuua yule mtu aliye mwachia aondoke"

uhai wake utachukuliwa

Hii ni njia ya heshima kumrejea mtu aliyeuawa. "tutachukua uhai wake" au "tutamuua"

kwa kuwa wa yule

"katika kubadilishana uhai wa uyo mtu" Hapa huyu mtu inarejea kwa "uhai" wake, kusisitiza kwamba hakuwa amekufa. "kwa kuwa huyo mtu"

2 Kings 10:25

aliwaambia mlinzi na manahodha

Yehu alitoka nje ya hekalu kabla ya kunena na mlinzi. "alirudi nje ya hekalu la Baali na kuwaambia walinzi na manahodha"

kwa ukali wa upanga

Kisha watu wakatumia panga kuwaua wamwabuduo Baali. Hili neno linarejea kwa panga zao. "pamoja na panga zao" (UDB)

wakawatupa nje

Hii inamaanisha kwamba walizitupa maiti nje za watu ya hekalu. "walizitupa maiti zao nje ya hekalu"

kuifanya choo

"kuifanya choo cha uma" Choo ni chumba cha kuogea, au eneo la choo, kawaida kwa ajili ya kambi au majengo yalitumika kwa nyumba ya maaskari.

ambacho kipo hadi leo

Hii inamaanisha kwamba hicho kitu kilichosalia katika hali flani hadi wakati huu. "na tangu hapo ilikuwa hivyo siku zote"

2 Kings 10:29

hakuacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati

Hii inamzungumzia Yehu akifanya dhambi zile zile ambazo Yeroboamu alizozifanya, kana kwamba dhambi za Yeroboamu zilikuwa sehemu ambayo Yehu hakuziacha. "hakuacha kufanya aina ya dhambi ambazo Yeroboamu mwana wa Nabeti alizifanya" (UDB)

Nabeti

Hili ni jina la kiume

dhambi ya Israeli

Hapa "Israeli" inarejea kwa watu walioshi huko. "dhambi ya watu wa Israeli"

katika kutimiza

"katika kutekeleza" au "katika kukamlisha"

kile kilicho sahihi katika macho wangu

Macho yanawakilisha kuona, na kuona kunawakilisha mawazo au hukumu. "Kile nilichohukumu kuwa sahihi" au "kile nifikiriacho kuwa sawa"

nyumba ya Ahabu

Hapa "nyumba" ya Ahabu inarejea kwa "familia" yake." "familia ya Ahabu"

yote hayo yalikuwa katika moyo wangu

Hapa "moyo" unawakilisha "tamaa" "yote ninayoyatamani kwa ajili yako kufanya" au "yote ambayo ninayoyataka uyafanye"

kukaa juu ya kiti cha kifalme

"kuwa wafalme"

hata kizazi cha nne

"hata kizazi cha 4" au "kwa vizazi vinne vijavyo." Hii inarejea kwa mwana wake, mjukuu, kitukuu, na nyanya.

Yahwe hakuwa makini kutembea katika sheria ya Yahwe

Hapa "kutembea" inarejea kwa "kuishi." "Yehu hakuwa makini kuishi kulingana na sheria ya Yahwe"

kwa moyo wake wote

Hapa "moyo" inarejea kwa matashi ya mtu na tamaa. "katika kila kitu alichokifanya"

Hakuzigeukia dhambi za Yeroboamu

Ku "geukia" kutoka kwenye kitu inamaanisha kuacha kukifanya. "Yehu hakuacha kufanya dhambi kama alivyofanya Yeroboamu"

2 Kings 10:32

kupunguza mikoa ya Israeli

"kuanza kusababisha himaya iliyotawaliwa na Israeli kuwa ndogo"

mikoa

"maeneo ya nchi"

Hazaeli kuwashinda

Hapa "Hazaeli" inamrejea mwenyewe na jeshi lake. "Hazaeli na jeshi lake"

Hazaeli

Hili lilikuwa jina la kiume

kutoka magharibi mwa Yordani

"kutoka kwenye nchi mashariki ya Yordani"

Aroeri ... Bashani

Haya yote ni majina ya sehemu.

Arnoni

"Mto Arnnoni" Hili ni jina la mto.

2 Kings 10:34

je hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli?

Hili ni swali lisilohitaji majibu linaloweza kuandikwa kama sentensi. "yameandikwa kwenye Kitabu cha matukio ya Wafalme wa Israeli."

Yehu akalala na wazee wake, na walimzika katika Samaria

Hii inamaanisha kwamba yehu alikufa. Hii inazungumzia yeye kuzikwa walipozikwa wazee wake kana kwamba alikuwa amelala pamoja nao. "Yehu akafa na kuzikwa katika Samaria, ambapo pia walizikwa wazee wake."

Yehoahazi

Hili ni jina lwa mwanamume.

Mda ambao Yehu alitawala juu ya Israeli katika Samaria ulikuwa miaka ishini na nane

miaka ishirini - "Yehu alitawala juu ya Israeli katika Samaria kwa mda wa miaka ishirini na nane"

miaka ishirini na nane

miaka minane - "miaka 28"

2 Kings 11

2 Kings 11:1

Athalia ... Yehosheba ... Yoashi

watoto wa mfalme

kuona kwamba mtoto wake alikuwa amekufa

"kuwa makini kwamba mtoto wake alikuwa amekufa"

aliinuka na kuwaua watoto wote wa kifalme

Athalia hakuwaua watoto mwenyewe. "aliwaamuru watumishi wake kuwaua idadi yote ya familia ya Ahazia walioweza kuwa wafalme"

akamchukua Yoashi mwana wa Ahazia, na kumficha mbali mwa miongoni mwa watoto wa mfalme waliokuwa wameuawa, wakati wote pamoja na mlezi wake; akawaweka kwenye chumba cha kulala. Wakamficha kutoka Athalia kwa hiyo hakuuawa

"akamchukua mtoto mdogo sana wa Ahazia Yoashi na kumficha na mhudumu wake katika chumba cha kulala katika hekalu. Hivyo hakuuawa." (UDB)

Alikuwa pamoja na Yehosheba, wamejificha kwenye nyumba ya Yahwe, kwa mda wa miaka sita, wakati Athalia alipotawala juu ya nchi

Hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji. "Yoashi na Yehosheba alijificha miaka sita katika nyumba ya Yahwe kama Athalia alivyoongoza nchi"

nchi

"ufalme"

2 Kings 11:4

Kauli Unganishi:

Hii inaendelea hadithi ya kilichotokea baada ya Yoashi, mwana wa Mfalme Azaia, alijificha kwenye hekalu baada ya Wafalme wote wa uzao wa Ahazia kuawa.

Katika siku ya saba

"Katika siku ya saba ya utawala wa Athalia" au "Katika mwaka wa 7 wa utawala wa Athalia"

Yehoyada

kuhani mkuu

Wakari

Hili ni jina la kundi maalumu la walinzi wa kifalme.

kuwaleta kwake

Yehoyada, kuhani mkuu, alikuwa na hawa askari wa kijeshi wakitoa taarifa kwake kwenye hekalu. "walikuja kuonana naye kwenye hekalu"

Kisha akawaonyesha mwana wa mfalme

Yehoyada akawafunulia kwamba Yoashi, mwana wa Mfalme Azahia, alikuwa bado yu hai.

2 Kings 11:7

Maelezo ya Jumla:

Yehoyada anaendelea kutoa mwelekeo kwa maaskari ambao watamlinda Mfalme Yoashi.

kwa ajili ya mfalme

Walitakiwa waendelee kuangalia kwa lengo la kumlinda mfalme kuumizwa. "ili kumlinda Mfalme Yoashi"

Yeyote aingiaye ndani ya safu yako

Safu inarejea mstari wa maaskari. "Yeyote aingiaye kwenda nyuma yako wakati unamlinda Mfalme Yoashi"

acha auawe

Hii inaweza kuanza katika muundo tendaji. "lazima umuue"

Lazima mkae pamoja na mfalme kila atokapo na kila aingiapo

Haya mambo mawili ya kinyume ni uaminifu ambayo yanarejea kwa kila kitu mfalme afanyacho. "Lazima ukae karibu na mfalme mda wote"

2 Kings 11:9

mamia ya makamanda

Hii inareje kwa maafisa waliowashangaza walinzi wa kifalme na walinzi wa nyumba ya kifalme.

Kila mmoja

"Kila kamanda"

ambayo katika nyumba ya Yahwe

"ilipokuwa imetunzwa kwenye hekalu"

2 Kings 11:11

kutoka upande wa kuume wa hekalu, kwenda upande wa kushoto, karibu na madhabahu ya hekelu

Haiko wazi kama neno "nyumba" hapa inarejea kwenye hekalu au jumba la kifalme.

kumleta nje mwana wa mfalme

Yehoyada, kuhani mkuu, akamleta mwana wa mfalme, Yoashi, nje kutoka kwenye hekalu la fleti ambapo alipokuwa amefufuka kwa kujificha.

kumpatia mikataba ya agano

"kumzawadia kwa kitabu cha sheria"

kumpaka mfuta

Kuhani alimwagiwa mafuta ya mzaituni juu ya kichwa cha Yoashi kama ishara kwamba sasa alikuwa mfalme. "kumwagiwa mafuta ya mzaituni juu ya kichwa cha Yoashi"' (UDB)

kupiga makofi

Kupiga makofi ilikuwa ishara ya furaha ya watu kwenye kupakwa mafuta ya mfalme mpya.

2 Kings 11:13

sauti ya mlinzi

Hii inarejea kwenye sauti iliyotengenezwa na maaskari wote.

alikuja kwa watu katika nyumba ya Yahwe

"alikuja mahali ambapo watu walipokuwa wakikusanyika kwenye hekalu"

Alitazama, na, tazama, mfalme alikuwa amesimama

Hapa "tazama" inasisitiza kwamba alishangazwa kumuona Yoashi. "Wakati alipofika, alishangazwa kumuona Mfalme Yoashi amesimama"

karibu na nguzo

"karibu na moja ya nguzo za hekalu"

kama utamaduni ulivyokuwa

"ambapo ilikuwa kawaida jumba kwa ajili mfalme kusimama"

tarumbeta

watu ambao wachezao tarumbeta

Athalia alirarua mavazi yake

Alirarua mavazi yake kuonyesha kwamba alikuwa alikuwa amekasirika sana na hasira.

Uhaini! Uhaini!

"Wewe ni mhaini! Umenisaliti!" (UDB)

2 Kings 11:15

mamia ya makamanda

Hii inarejea kwa maafisa waliosimamia walinzi wa kifalme na walinzi wa nyumba ya kifalme.

Mtoeni kwenye safu

Safu ni mistari au mstari wa maaskari.

Yeyote amfuataye

Inadokeza kwamba mtu aliyemfuata atakuwa anajaribu kumsaidia. "Yeyote anayemfuata kujaribu kumuokoa"

wakamtwaa kadiri walivyokuwa wakiikaribia hiyo sehemu iliyokuwa na farasi wakaingia chini, na akauawa huko

Baadhi ya matoleo yanatafsiri hii kama "walinzi wakamtwaa na kumchukua hadi kwenye jumba la kifalme, hadi kwenye jumba la kifalme ambapo farasi huingia kwenye ua."

2 Kings 11:17

pia kati ya mfalme na watu

"pia kutengeneza agano kati ya mfalme na watu"

watu wote wa nchi

Huku ni kuenea kuonyesha kwamba kundi kubwa la watu walilia chini kwenye hekalu la Baali. idadi kubwa ya watu wa nchi"

nyumba ya Baali

"hekalu la Baali"

Matani

Hili ni jina la kuhani wa kiume.

2 Kings 11:19

Maelzo ya Jumla:

Wamemchukua mfalme mpya, Yoashi, kutoka kwenye hekalu hata kwenye nyumba ya mfalme.

mamia ya makamanda

Hii inareje kwa maafisa waliowashangaza walinzi na walinzi wa nyumba ya mfalme.

Wakari

Hili ni jina la kundi maalumu la walinzi wa kifalme.

wakamleta chini mfalme kutoka kwenye nyumba ya Yahwe na wakaenda kwenye nyumba ya mfalme

"kumleta mfalme kutoka kwenye hekalu hadi kwenye nyumba ya mfalme"

watu wote wa nchi furahini

Hii ni kujumuisha. Inawezekana kwamba wengine hawakufurahi.

mji ulikuwa kimya

"mji ulikuwa shwari" au "mji ulikuwa na amani"

2 Kings 11:21

Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba

"Yoashi alikuwa na umri wa miaka 7"

2 Kings 12

2 Kings 12:1

Katika siku ya saba ya Yehu

"Kipindi cha mwaka wa 7 wa utawala wa Yehu juu ya Israeli"

utawala wa Yoashi ulianza

"Yoashi alianza kutawala juu ya Yuda"

Sibia

Hili lilikuwa jina la mwanamke.

Sibia, wa Bersheba

"Sibia, kutoka mji wa Bersheba" (UDB)

kile kilicho sahihi usoni mwa Yahwe

Neno "uso wa Yahwe" linawakilisha asili ya Yahwe. "kile kilichokuwa kinampendeza Yahwe"

kumwelekeza

"kumfundisha"

Lakini mahali za juu hazikuwa pamechukuliwa

Hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji. "Lakini watu hawakuziharibu mahali za juu"

Watu wakaendelea kutoa sadaka na kuchoma ubani kwenye sehemu za juu

Yahwe aliwakataza watu kuabudu katika hizi sehemu. Hii inaweza kuwa wazi. "Watu waliendelea kwenda sehemu ambazo hazikukubaliwa na Yahwe, kufanya dhabihu na kuchoma ubani"

2 Kings 12:4

pesa zote zilizokuja kama sadaka takatifu kwenye nyumba ya Yahwe

Hii inazirejea pesa ambazo watu huto kusaidia hekalu. Hizi pesa huja katika miundo mitatu ambayo zimeelezwa katika mwisho wa sentensi.

pesa zilizoletwa na watu zilimuhasisha Yahwe katika mioyo yao kutoa

Hii inazirejea pesa ambazo watu waliamua kuzitoa kwa uhuru kwa Yahwe.

2 Kings 12:6

karibu na mwaka wa ishirini na tatu wa Mfalme Yoashi

mwaka wa tatu wa Mfalme Yoashi* - "wakati Yoashi alipokuwa mfalme kwa miaka ishirini na tatu"

Kwa nini hujakarabati kitu chochote kwenye Hekalu?

Yoashi anauliza hili swali kuwakemea makuhani. "Mlitakiwa muwe mmekarabati hekalu!"

wapatie wale ambao wanweza kufanya ukarabati.

"kulipa watenda kazi watakaofanya ukarabati"

2 Kings 12:9

Badala yake

"Badala ya makuhani kukusanya pesa"

upande wa kulia kama mtu anaingia kwenye madhabahu ya Yahwe

"upande wa kulia wa kuingia kwenye hekalu"

weka kwenye

"weka kwenye kasha" au "kuweka kwenye sanduku" (UDB)

pesa ambazo zilizokuwa zimeletwa

Hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji. "pesa ambazo watu walizileta"

kuweka pesa katika mfuko na kisha kuzihesabu

Matoleo mengi yanaiweka hii katika mpango wa mantiki kama vile "kuhesabu pesa na kuziweka katika mifuko."

weka pesa kwenye mifuko

Maana ziwezekanazo ni 1) "kuweka pesa katika mifuko" au 2) "kufunga pesa juu katika mifuko" (UDB).

pesa zilipatikana

"pesa zilizokuwa zimepatikana katika kasha"

2 Kings 12:11

imepimwa

"imehesabiwa"

kwenye mikono ya watu

Hapa "mikono" inarejea kwa watu. "kwa watu"

waliokuwa wanatunza hekalu

"waliokuwa wanakarabati hekalu"

maseremala

watu wajengao na kukarabati vitu vilivyotengenezwa kwa mbao

waashi

watu wajengao kwa mawe

wakata mawe

watu wakatao mawe kwenye kipimo kimoja na umbo

kwa ajili ya kununua mbao na kukata mawe

"kununua mbao na kukata jiwe"

yote iliyokuwa inahitajika kulipwa kwa ajili ya kuitengeneza

"kulipa kwa ajili ya ukarabati wote"

2 Kings 12:13

haikulipwa kwa kufanya chochote

"hazikutumika kulipwa kwa ajili ya sehemu yoyote ya hekalu"

vikombe vya fedha, mabeseni, au dhahabu au fedha yoyote ya vyombo

Hivi ni vitu ambavyo vilikuwa vitumike na makuhani kwa ajili ya kazi mbali mbali, kama vile dhabihu au sikukuu.

2 Kings 12:15

hazikuzihitajika zile pesa zilipwe kwa ajili ya matengenezo ili kuhesabiwa kwa ajili ya watu waliozipokea nakuzilipa kwa watenda kazi

Hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji. "hawakuwataka watu waliopokea pesa na kuwalipa watenda kazi kwa ajili ya kukarabati kuhesabu pesa"

kuwajibika kwa ajili ya

kuendelea kuhifadhi ni kiasi gani cha fedha kilichokuwa kimepokewa na kutumika

pesa kwa ajili ya matoleo ya hatia na pesa kwa ajili ya matoleo ya dhambi hazikuwa zimeletwa kwenye hekalu la Yahwe

Inaelezwa kwamba hizi pesa hazikutumika kwa ajili ya ukarabati. Hii inaweza kuelzwa katika muundo tendaji. "hawakutumia pesa kutoka kwenye sadaka za hatia na sadaka za dhambi kulipa kwa ajili ya kukarabati hekalu la Yahwe"

2 Kings 12:17

Hazaeli mfalme wa Shamu akatekwa ... Hazaeli akarudi kuishambulia

Hii inarejea kwa jeshi la Hazaeli pia kama kwa Hazaeli. "Hazaeli mfalme wa Shamu na jeshi lake wakashambuliwa ... Kisha wakarudi kushambulia"

Hazaeli

Hili ni jina la mfalme wa nchi ya Siria.

kuichukua

"kushinda na kuitawala"

Yehoshafati na Yehoramu na Ahazia, baba zake

Hawa watu walikuwa wafalme waliopita wa yuda.

iliyotengwa

"weka wakfu"

dhahabu iliyokuwa imepatikana katika vyumba vya kuhifadhi"

"dhahabu ambayo ambayo ilikuwa imehifadhiwa kwenye vyumba vya kuhifadhi"

Kisha Hazaeli akaondoka kutoka Yerusalemu

Zawadi Yoashi alizompatia Hazaeli zilimshawishi asiishambulie Yerusalemu. Hii inaweza kuwekwa wazi. "Basi Hazaeli aliacha kuishambulia Yerusalemu na kuondoka"

2 Kings 12:19

je hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Yuda?

Hili swali linatumika kumkumbusha msomaji kwamba haya mambo yamerekodiwa. "yameandikwa katika kitabu cha historia ya Wafalme wa Yuda."

Sila

Eneo la hii sehemu haijulikani.

Yozakari ... Shimeathi ... Yehozabadi ... Shomeri ... Amazia

Haya ni majina ya wanaume.

pamoja na baba zake

"katika jumba la kifalmeambapo baba zake walipokuwa wamezikwa (UDB)

akawa mfalme katika mahali pake

"akawa mfalme wa Yuda aliyefuata"

2 Kings 13

2 Kings 13:1

Katika mwaka wa ishirini na tatu wa Yoashi mwana wa Ahazia mfalme wa Yuda

mwaka wa tatu wa Yoashi mwana wa Ahazia mfalme wa Yuda - "Baada ya Yoashi alipokuwa akitawala Yuda kwa takribani miaka 23"

kutawala juu ya Israeli katika Samaria

"tawala juu ya ufalme wa Israeli iliyopo katika Samaria"

alitawala miaka kumi na saba

"Yehoahazi alikuwa mfalme kwa miaka 17"

Alifanya yale yaliyo maovu usoni mwa Yahwe

Hapa "katika uso wa" inarejea kwa maoni ya Yahwe. "Alifanya yale yaliyo maovu kulingana na Yahwe"

kufuata dhambi za Yeroboamu

"kufanya dhambi zile zile kama Yeroboamu"

Yehoahazi hakugeuka kutoka kwao

Hapa kusimama dhambi yake inazungumziwa kana kwamba amerudi kutoka kwao. Hii pia inaweza kuelezwa katika muundo chanya. "Yehoyazi hakuacha kufanya dhambi za Yeroboamu" au "Yehoyazi aliendelea kufanya dhambi zile zile kama Yeroboamu"

2 Kings 13:3

Hasira ya Yahwe ikawaka juu ya israeli

Yahwe kuwa na hasira na Israeli inazungumziwa kana kwamba hasira yake ilikuwa moto uliokuwa unawaka. "Kisha Yahwe akawa na hasira sana na Israeli"

akaendelea kuwakabidhi kwenye mikono ya Hazaeli mfalme wa Shamu na kwenye mikono ya Ben Hadadi mwana wa Hazaeli

Hapa "wao" inarejea kwa Israeli na "mkono" inarejea kwenye nguvu kuwatawala. "kumruhusu Hazaeli mfalme wa Shami, na Ben Hadadi, mwanaye, kuwashinda mara kwa mara Waisraeli katika vita"

kumsihi Yahwe

"kumuomba Yahwe"

aliona mateso ya Israeli, vile mfalme wa Shamu alivyokuwa akiwatesa

Haya maneno mawi yanamaaanisha kitu kimoja na yamerudiwa kusisitiza. "ukandamizaji" inamaanisha kama "mfalme wa Shami alivyokuwa akiwakandamiza."aliona mara kwa mara mfalme wa Shami alikuwa akiwakandamiza Israeli"

mkombozi

"mtu wa kuwaokoa"

walikimbia kutoka kwenye mkono wa Washami

Hapa "mkono" unarejea kwa nguvu ya kuwatawala. "aliwawezesha kuwa huru kutoka nguvu ya Shami"

2 Kings 13:6

hawakuziacha dhambi za nyumba ya Yeroboamu

Kuacha kufanya dhambi kunazungumziwa kana kwamba waliondoka kutoka kwenye dhambi. "Israeli hawakuacha kufanya dhambi zile zile kama Yerobamu alizokuwa amezifanya" au "Israeli iliendelea kufanya dhambi zile zile kama Yeroboamu alizokuwa amezifanya"

nyumba ya Yeroboamu

"familia ya Yeroboamu"

aliwaangamiza

"alilishinda jeshi la Yehoahazi"

kuwafanya kama makapi yaliyopurwa

Jeshi la Washami liliwashinda moja kwa moja jeshi la Israeli ambacho kilichokuwa kimebaki hakikuwa na thamani ambacho kinalinganishwa na makapi ya ngano ambayo wafanya kazi hutembea kwenye kipindi cha mavuno. "aliwaangamiza kama wafanyakazi waangamizavyo makapi chini ya miguu yao wakati wa mavuno"

2 Kings 13:8

je hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli?

Hili swali limetumika kumkumbusha msomaji kwamba matendo ya Yehoahazi yameandikwa kwenye kitabu kingine. Ona jinsi hili neno lilivyotafsiriwa katika 1:17. "yameandikwa katika Kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli."

akalala na mababu zake

Hii ni njia ya heshima ya kusema kwamba amekufa.

2 Kings 13:10

Katika mwaka wa thelathini na saba wa Yoashi mfalme wa Yuda

mwaka wa saba wa Yoashi mfalme wa Yuda - "Baada ya Yoashi kutawala Yuda kama miaka 37"

utawala wa Yoashi mwana wa Yehoashi ulianza juu ya Israeli katika Samaria

"Yehoashi mwana wa Yehoahazi alianza kutwala juu ya Israeli katika Samaria"

Yehoashi

Huyu alikuwa mfalmew aIsraeli ambaye alikuwa mwana wa Yehoahazi.

Alifanya yaliyo maovu usoni mwani Yahwe

Hapa "uso" unawakilisha mwazo wa Yahwe au hukumu. "Alifanya mambo ambayo Yahwe aliyoyafikiria kuwa uovu"

Hakuacha nyuma dhambi zake zozote za Yeroboamu

Kuacha kufanya dhambi inzungumziwa kana kwamba aliacha dhambi nyuma" Hii inaweza kuelezwa katika muundo chanya. "Yoashi hakuacha kutenda dhambi kama Yeroboamu" "Yoashi aliendelea kufanya dhambi kama dhambi za Yeroboamu"

ambayo aliifanya Israeli kuasi

"ambayo Yeroboamu aliifanya Israeli kuasi"

lakini alitembea katikati yao

Kutenda dhambi kunzungumziwa kana kwamba alikuwa akitembea karibu na njia ya dhamb. "lakini Yoashi anaendelea kufanya dhambi hizi hizi"

2 Kings 13:12

na shujaa wake ambaye aliyepigana dhidi ya Amazia mfalme wa Yuda

"na nguvu ambayo jeshi lake ilionyesha wakati walipokuwa wakipigana juu ya jeshi la Amazia mfalme wa Yuda"

je hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli?

Hili swali linatumika kumkumbusha msomaji kwamba matendo ya Yehoahazi yaliandikwa katika kitabu kingine. Taza jinsi ambavyo ilivyotafsiriwa katika 1:17. "yameandikwa katika kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli."

Yehoashi akalala na babu zake

"Hii ni njia ya heshima kusema Yehoashi amekufa.

Yeroboamu alikaa juu yakiti chake

Hapa "alikaa juu ya kiti chake" inarejea kutawala kama mfalme. "Yeroboamu akawa mfalme baada ya yeye" au "Yeroboamu akaanza kutawala baada ya yeye"

2 Kings 13:14

omboleza juu yake

"omboleza kwa sababu Elisha alikuwa anaumwa"

Baba yangu, baba yangu

Elisha hakuwa baba wa mfalme halisi. Mfalme Yoashi alitumia hili neno kama alama ya heshima.

magari ya farasi ya Israeli na hawa waendesha farasi wanakuchukua

Hii ni kumbukumbu kwa Elisha kwanda mbinguni katika 2:11. Yoashi anatumika hili neno kusema kwamba Elisha alikwa anaenda kufa. "magari ya farasi ya Israeli na waendesha farasi wanakuchukua kwenda mbinguni"

waendesha farasi

Hii inarejea kwa watu waliokuwa wakiendesha farasi. "waendesha magari ya farasi"

2 Kings 13:17

Maelezo ya Jumla:

Elisha anaendelea kuongea na Yoashi, mfalme wa Israeli.

Fungua dirisha upande wa mashariki

"fungua dirisha lielekee mashariki" au "fungua hilo dirisha kuelekea mashariki" (UDB)

hivyo alilifungua

Tangu hii ilipotokea baada ya Yoashi kuchukua upinde na mishale, inaweza kuwa alikuwa mtumishi wa kufungua dirisha.

akarusha

"Yoashi akarusha mshale"

Huu ndiyo mshale wa ushindi wa Yahwe, huu mshale wa ushindi juu ya Shamu

Mahusiano kati ya mshale na ushindi unaweza kuwekwa wazi. "Huu mshale ni alama kutoka kwa Yahwe ambao atakupatia ushindi juu ya Shami"

Afeki

Huu ulikuwa mji katika nchi ya Israeli.

Lakini mtu wa Mungu alikuwa na hasira naye

"Lakini Elisha alikuwa na hasira na Mfalme Yoashi"

hadi ulipoingamiza

"hadi ulipoiangamiza kabisa"

2 Kings 13:20

Sasa

"Wakati ule"

mwanzoni mwa mwaka

"kila mwaka majira ya machipuko" (UDB)

Walipokuwa wakimzika mtu flani

"Kama baadhi ya Waisraeli walipokuwa wakiuzika mwili wa mtu"

waliona kundi la Wamoabu

Inaweza kuwekwa wazi kwamba walikuwa wakiogopa Wamoabu. "waliona kundi la Wamoabu washambuliaji wakija kuwaelekea na waliogopa"

kaburi la Elisha

"kaburi ambalo Elisha alizikwa"

Mara yule mtu alipoigusa mifupa ya Elisha

Hapa "mtu" inarejea kwa maiti yake. Hii inaweza kuwekwa wazi. ""Mara alipokufa mwili wake uliigusa mifupa ya Elisha"

alifika na kusimama kwa miguu yake

"maiti ya mtu ilifufuka na kusimama juu"

2 Kings 13:22

Lakini Yahwe aliwahurumia Israeli, na alikuwa na huruma juu yao na kushuhulika kwa ajili yao

Inaweza kuwa msaada kugawanya sentensi yake kwenye sehemu ndogo ndogo. "Lakini Yahwe alikuwa mkarimu sana kwa watu Waisraili. Aliwasaidia" (UDB)

Hivyo Yahwe hakuwaangamiza

Agano ya Yahwe ni sababu hakuiangamiza Israeli. Hii inaweza kuwekwa wazi. "Hii ni sababu kwamba Yahwe hakuwaangamiza" au "Kwa sababu ya agano lake, Yahwe hakuwaangamiza"

hakuwatupa kutoka kwenye uwepo wake

Kukataa kwa Yahwe kunazungumziwa kana kwamba alikuwa akiitoa Israeli kwa mwili kutoka alipokuwa. "hakuwakataa" (UDB)

2 Kings 14

2 Kings 14:1

Katika mwaka wa pili wa Yehoashi mwana wa Yehoazi, mfalme wa Israeli

"wakati Yehu mwana wa Yehoazi alipokuwa mfalme wa Israeli takribani miaka miwili"

Amazia mwana wa Yoashi, mfalme wa Yuda, akaanza kutawla

Amazia mwana wa Yoashi, akawa mfalme wa Yuda"

Alikuwa na umri wa miaka ishirini na tano alipoanza kutawala

miaka ishirini na tano wakati alipoanza kutawala - "Alikuwa na umri wa miaka 25 alipokuwa mfalme"

alitawala miaka ishirini na tisa katika Yerusalemu

miaka tisa katika Yerusalemu - "alikuwa mfalme katika Yerusalemu kwa miaka 29"

Yehoyadani

hili ni jina la mwanamke

Alifanya yaliyo sahihi katika uso wa Yahwe, sio kama Daudi baba yake

Hapa "usoni mwa Yahwe" inaurejea uso wake, na uso wake unarejea hukumu yake. "Amazia alifanya mambo mengi yaliyompendeza Yahwe, lakini hakufanya mambo mengi ambayo yalimtukuza Yahwe kama mfalme Daudi aliyokuwa ameyafanya"

Alifanya kila kitu ambacho Yoashi, baba yake, alifanya

Yoashi alimtii Yahwe na kufanya mambo mazuri. "Alifanya baadhi ya mambo mazuri ambayo baba yake Yoashi aliyafanya"

2 Kings 14:4

Maelezo ya Jumla:

Hadithi ya kanuni ya Amazia kama mfalme wa Yuda inaednelea.

Lakini mahali pa juu hapakuwa pamechukuliwa

Mahali pa juu palikuwa pakitumika kwa ajili ya kuabudu kipagani. "Lakini hakupaondoa mahali pajuu"

kutoa sadaka na kufukiza ubani hapo mahali pa juu

"Mahali pa juu palitumika kwa ajili ya kuabudu kipagani. "kutoa sadaka na kufukiza ubani kwa miungu ya kipagani mahali pa juu"

Ikawa mara

Hii inatumika kutambulisha tukio jipya.

mapema kama kanuni yake ilipokuwa imeanzishwa vizuri

"mapema kama Amazia alipotambulisha kanuni ya kifalme na mamlaka ya kifalme"

aliwaua watumishi

Amazia ni kama aliwaagiza watu wengine kuwaua maafisa. "aliwafanya watumishi wake kuwatekeleza maafisa" (UDB)

2 Kings 14:6

Maelezo ya Jumla:

Msimuliaji anaeleza kuhusu kile alichofanya mfalme Amazia baada ya baba yake Mfalme Yoashi kuuawa.

Ila hakuwaweka wana wa wauaji kwenye kifo

Mfalme Amazia hakuwaagiza watumishi wake kuwaua watoto wa watu waliomuua baba yao. "Lakini hakuwaambia watumishi wake kuwatekeleza hao watoto wa maafisa" (UDB)

Mababa wasiuawe kwa ajili ya watoto wao, wala watoto wasiuawe kwa ajili ya wazazi wao

"Watu wasiwaue mababa kwa ajili ya dhambi za watoto wao, na wasiwaue watoto kwa ajili ya dhambi za wazazi wao"

kila mtu atauawa kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe

"kila mtu atakufa kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe"

Aliwaua

Hapa "Yeye" inarejea kwa jeshi lake. "Jeshi la Amazia liliuawa" au " Maaskari wa Amazia waliuawa" (UDB)

maaskari elefu kumi

"maaskari 10,000"

Bonde la Chumvi

Hili ni jina la mahali panapoonyesha kusini mwa Bahari mfu.

pia aliichukua Sela katika vita

Hapa "Yeye" inarejea jeshi lake. "Jeshi la mfalme Amazia liliuchukua mji wa Sela

Sela ... Yoktheeli

Waliupa mji wa Sela. Jina jipya lilikuwa Yoktheeli.

2 Kings 14:8

Kisha Amazia akatuma wajumbe kwa Yehoashi mwana wa Yehoahazi mwana wa Yehu mfalme wa Israeli, akisema, "Njoo, tuonane kila mmoja macho kwa macho kwenye mashinadano."

Hapa "kila mmoja" kujumuisha na majeshi yao. "Kisha Amazia akapeleka wajumbe kwa Mfalme Yehoashi wa Israeli, akisema, "Njooni hapa tuyaache majeshi yetu yapigane katika vita" (UDB)

"Mbaruti uliokuwa Lebanoni ulituma kwa mwerezi katika Lebanuni ... umeanguka chini ya mbaruti

Hili ni neno la picha na fumbo. Mti wa mkangazi ni mkubwa na mbaruti ni mdogo na usio na thamani. Yehoashi anajilinganisha yeye na mkangazi na Amazia na mbaruti na kumuonya Amazia asimshambulie.

mbaruti

"kichaka chenye miba"

akisema, "Mtoe binti yako kwa mwanangu kuwa mke;

Hii nukuu ya moja kwa moja inaweza kuelezwa kama nukuu isiyo ya moja kwa moja. "kuuliza mkangazi kumtoa binti yake kwa mbaruti mwana wa mke"

Umemshambulia Edomu sana

Hii ni sehemu ya onyo la ujumbe wa Yuda kwa Amazia. "Amazia, umeishinda Edomu kabisa"

moyo wako umekuinua

Hii ni lugha ambayo inayorejea kuwa na kiburi. "una kiburi kwa kile ulichokifanya"

Chukua sifa katika ushindi wako

"Ridhika na ushindi wako"

kwa nini unataka kujisababishia matatizo na kuanguka

Yehoashi anatumia hili swali kumuonya Amazia asimshamulie.

2 Kings 14:11

Lakini Amazia hakutaka kusikia.

Hapa "kusikia" inarejea kutii onyo. "Ingawa, Amazia hakutii onyo la Yehoashi"

Hivyo Yehoashi mfalme wa Israeli akashambulia ... Amazia mfalme wa Yuda wakakuta uso kwa uso

Majeshi ya hawa wafalme yalienda kupigana nao. "Hivyo Yehoashi na jeshi lake wakaenda kupigana na Amazia na jeshi lake wakaonana uso kwa uso"

Bethi Shemeshi

Huu ni mji katika Yuda karibu na mpaka wa Israeli.

Yuda alishindwa na Israeli

"Israeli iliishinda Yuda"

kila mtu alikimbia nyumbani

"watu wote waliokuwa katika jeshi la Yuda walikimbia nyumbani"

2 Kings 14:13

Maelezo ya Jumla:

Hii ni jinsi ilivyotokea baada ya jeshi la Israeli kulishinda jeshi la Yuda huko Bethi Shemeshi.

Akaja ... Akachukua

Hapa "Yeye" inarejea kwa Yehoashi na jeshi lake. "Yehoyashi na jeshi lake wakaja ... maaskari wa Yehoyashi wakachukua"

lango la Efraimu ... pembe ya lango

Kuna majina ya malango katika ukuta wa Yerusalemu.

dhiraa mia nne

"kama mita 180"

dhiraa

Ridhaa moja ilikuwa kama sentimita 46.

pamoja na mateka pia, na kurudi Samaria

Hii inaonyesha kwamba Yehoyashi alihitaji kuchukua hawa mateka kumlinda Amazia asitekwe tena. Hii inaweza kuwekwa wazi. "na pia walimchukua baadhi ya wafungwa kuhakikisha kwamba Amazia asingewasababishia matatizo tena

2 Kings 14:15

je hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya mfalme wa Israeli?

Hili swali limetumika kumkumbusha msomaji kwamba matendo ya Yehoahazi yamehifadhiwa katika kitabu kingine. "yameandikwa katika Kitabu cha matukio ya wafalme wa Israeli."

Kisha Yehoashi akalala na wazee wake

Hii ni heshima kusema kwamba alikufa. "Kisha Yehoashi akafa"

akawa mfalme katika eneo lake

"akawa mfalme baada ya yeye"

2 Kings 14:17

je hayakuandikwa kwenye kitabu cha matukio ya mfalme wa Yuda?

Hili swali limetumika kuwakumbusha wasomaji kwamba haya mambo yamehifadhiwa. "yameandikwa katika kitabu cha historia cha Wafalme wa Yuda."

Wakafanya njama dhidi ya Amazia katika Yerusalimu

Njama ni mpango wa siri wa kuleta madhara kwa mtu au kitu. "Baadhi ya watu katika Yerusalemu walifanya njama juu ya Amazia"

Lakishi

Huu ni mji katika kusini ya magharibi mwa Yuda.

lakini walipeleka watu baada ya yeye kwenda Lakishi

Watu waliokuwa wametengeneza njama waliwatuma watu wengine kumfuata Amazia kwenda Lakishi.

2 Kings 14:20

Maelezo ya Jumla:

Hivi ndivyo ilivyotokea baada ya kifo cha Mfalme Amazia.

Wakamrudisha juu ya farasi

"Wakaurudhisha mwili wa Amazia juu ya farasi"

Watu wote wa Yuda wakamchukua Azaria, ambaye alikuwa na umri wa miaka kumi na minne, na walimfanya kuwa mfalme katika nyumba ya kifalme wa baba yake Amazia

Hii inajumiosha. Baadhi watu wanaweza wasimtake kuwa mfalme. "Watu wa Yuda walimchukua Azaria akiwa na miaka 16 na kumfanya kuwa mfalme baada ya baba yake, Amazia"

Alikuwa Azaria aliyeijenga Elathi

Azaria hakulifanya hili peke yake. "Alikuwa Azaria aliyemwagiza Eliathi kujengwa" au "Alikuwa Azaria aliyesimamia kujengwa tena kwa Eliathi"

Azaria

Huyu mfalme anafahamika sasa kwa jina la Uzia."

Eliathi

mji mmoja katika Yuda

kuirudishia Yuda

"kuirejesha ka Yuda"

kulala na wazee wake

Hii ni heshima kusema alikufa.

2 Kings 14:23

Maelezo ya Jumla:

Hii inaeleza kile Mfalme Uzia alichokifanya baada ya kuwa mfalme.

Katika mwaka wa kumi na tano wa Amazia

"katika mwaka wa 15 wa Amzia"

miaka arobaini na moja

mwaka mmoja - "miaka 41"

uovu katika uso wa Yahwe

Hapa "uso" ni picha kwa ajili ya kuhukumu. "uovu kulingana na Yahwe"

Hakuziacha dhambi yoyote ya kutoka kwa Yeroboamu

Kuacha kuasi imezungumziwa kama kupita njia. Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji. "Hakuacha kufanya dhambi kama dhambi za Yeroboamu" au "Aliendelea kufanya dhambi kama dhambi za Yeroboamu"

Akarudisha mipaka

Hii inamaanisha jeshi lake lilirudisha nchi hata kwenye mpaka. "Maaskari wake wakayashinda baadhi ya maeneo yaliyokuwa yamemilikiwa na Israeli"

Lebo Hamathi

Huu mji pia ulikuwa unaitwa Hamathi.

Bahari ya Araba

"Bahari mfu" (UDB)

2 Kings 14:26

yalikuwa machungu sana

Kuteseka ilikuwa vigumu ilizungumziwa kana kwamba ilikuwa ladha chungu. "ilikuwa chungu sana"

hapakuwa na mwokozi kwa ajili ya israeli

"hapakuwa na mtu yeyote angeweza kuiokoa israeli"

kufuta

Kuiangamiza Israeli kabisa inazungumziwa kana kwamba Yahwe amewasafisha kwa nguo. "angamiza kabisa"

jina la Israeli

Hapa "jina la Israeli" linawakilisha Israeli yote na wenyeji wake. "watu wa Israeli"

chini ya mbingu

"juu ya nchi"

aliwaokoa kwa mkono wa Yeroboamu mwana Yehoashi

Hapa "mkono" unarejea kwa uweza. Yeroboamu aliwashinda maadui wa Israeli kwa msaada wa jeshi lake. "alimuwezesha Mfalme Yeroboamu na jeshi lake kuwaokoa"

2 Kings 14:28

Je hayajaandikwa katika Kitabu cha matukio ya Wafalme wa Israeli?

Hili swali limetumika kumkumbusha msomaji kwamba matendo ya Yehoyazi yamehifadhiwa katika kitabu kingine. "yameandikwa katika Kitabu cha matukio ya Wafalme waa Israeli.

Yeroboamu akalala na wazee wake, pamoja na wafalme wa Israeli

Hii ni njia ya heshima kusema kwamba alikufa na alizikwa. "Yeroboamu akafa, na alizikwa walipokuwa wamepelekwa wafalme wengine wa Israeli walipozikwa"

2 Kings 15

2 Kings 15:1

Katika mwaka wa ishirini na saba wa Yeroboamu

Mwaka wa saba wa Yeroboamu - huu ni mwaka wa ishirini na saba wa utawala wake. "Katika mwaka wa 27 wa utawala wa Yeroboamu"

Azaaria

Huyu mfalme anajulikana vizuri leo kwa jina la Uziya."

Yekolia

Hili ni jina la mama yake na Amazia

Alifanya yaliyo sahihi

"Amazia alifanya yaliyo sahihi"

yaliyo sahihi katika macho ya Yahwe

Neno "macho ya Yahwe" linasimama kwa ajili ya uso wa Yahwe, ambao ni badala ya hukumu ya Yahwe. "yaliyo sahihi katika hukumu ya Yahwe"

2 Kings 15:4

mahala pa juu hapakuwa pameondolewa

"hakuna aliyepaondoa mahali pa juu" au "Azaria hakuwa na yeyote wa kupaondoka mahali pa juu"

hapakuchukuliwa

Kuchukuliwa inawakilisha kuharibiwa. "paliharibiwa"

hata siku yake ya kufa

"kifo" "kufa" "hata siku aliyokufa"

Yothamu, mwana wa mfalme, alikuwa juu ya kaya

Neno "kaya" linarejea kwa watu waishio katika nyumba ya kifalme. Kwa sababu Azaria alikuwa na ukoma, alitakiwa aishi katika nyumba iliyojitenga. Hivyo mwana wake, Yothamu, akachukua shtaka juu ya nyumba ya kifalme.

alikuwa juu ya kaya

Kuwa juu ya kaya inawakilisha kuwa na mamlaka juu ya walio humo. "alikuwa kiongozi wa kaya" au "alikuwa na mamlaka juu ya wale walio katika nyumba ya Hazaria"

2 Kings 15:6

je hayajaandikwa ... Yuda?

Hili swali limetumika pengine kufahamisha au kukumbusha wasomaji kwamba habari kuhusu Azaria zipo katika hiki kitabu. "yameandikwa ... uda."

Azaria akalala na wazee wake

Kulala inawakilisha kufa. "Azaria alikufa kama wazee wake" au "kama wazee wake, Azaria alikufa"

walimzika pamoja na wazee wake

"familia yake ilimzika walipozikwa wazee wake walipokuwa wamezikwa"

akawa mfalme katika mahali pake

Neno "katika mahali pake" ni sitari ikimaanisha "badala yake." "akawa mfalme badala ya Azaria"

2 Kings 15:8

Katika mwaka wa thelathini na nane wa Azaria mfalme wa yuda

mwaka wa nane wa Azaria mfalme wa Yuda - Inaweza kuelezwa wazi kwamba hii ni miaka thelathini na nane mwaka wa utawala wake. "Katika mwaka wa 38 wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda"

Zakaria mwana wa Yeroboamu

Huyu Yeroboamu alikuwa mfalme wa pili wa Israeli ambaye alikuwa na hilo jina. Alikuwa mwana wa mfalme Yoashi.

alitawala juu ya Israeli katika Samaria kwa miezi sita

Samaria ni mji ambao Zekaria aliishi huko alipokuwa mfalme wa Israeli. "aliishi Samaria na kutawala juu ya Israeli kwa miezi sita"

Alifanya yaliyo maovu

"Zekaria alifanya yaliyo maovu"

yaliyo maovu katika uso wa Yahwe

Uso wa Yahwe unawakilisha hukumu ya Yahwe. "yaliyo maovu katika hukumu ya Yahwe" au "kile Yahwe afikiriacho kuwa uovu"

Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nabeti

Kuziacha`dhambi inawakilisha kuzifanya hizo dhambi. "Zekaria hakukataa kufanya dhambi za Yeroboamu mwana wa Nabeti" au "aliasi kama Yeroboamu mwana wa Nabeti alivyo asi"

Yeroboamu mwana wa Nabeti

Huyu Yeroboamu alikuwa mfalme wa kwanza kati ya makabila kumi ya kaskazini ambayo yaliutengeneza ufalme wa Israeli.

ambaye aliisababisha Israeli kuasi

Hapa neno "Israeli" linawakilisha watu wa ufalme wa Israeli. "ambao walisababisha watu wa Israeli kuasi"

2 Kings 15:10

Shalumu ... Yabeshi

Haya ni majina wanaume.

Zekaria

"Mfalme Zakaria"

Ibleamu

Hili lilikuwa jina la mji.

Kisha akawa mfalme katika mahali pake

"Kisha Shalumu akawa mfalme katika mahali pa Zekaria"

yameandikwa katika Kitabu cha Matukio ya Wafalme wa Israeli

"mnaweza kuyasoma katika Kitabu cha Matukio ya Wafalme wa Israeli"

Kisha akawa mfalme katika mahali pake

"Kisha Shalumu akawa mfalme katika mahali pa Zekaria"

Uzao wako utaketi juu ya kikti cha Israeli hata kizazi cha nne

Kukaa juu ya kiti inawakilisha kuwa mfalme. "Uzao wako utakuwa wafalme wa Israeli kwa vizazi vinne"

2 Kings 15:13

katika mwaka wa thelathini na tisa wa Azaria mfalme wa Yuda

mwaka wa tisa wa Azaria mfalme wa Yuda - Inaweza kuelezwa wazi kwamba huu ni mwaka wa thelathini na nane wa utawala wake. "katika mwaka wa 39 wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda"

Shalumu ... Yuda

Haya ni majina ya wanaume.

Menahemu ... Gadi

Haya ni majina ya wanaume wawili.

alitawala mwezi mmoja pekee katika Samaria

Samaria ni mji ambao aliishi alipokuwa mfalme wa Israeli. "Shalumu aliishi katika Samaria na kutwala juu ya Israeli kwa mda wa mwezi mmoja tu"

akawa mfalme katika mahali pake

Neno "katika mahali pake" ni sitiari inayomaanisha "badala yake." "kuwa mfalme badala ya Shalumu"

2 Kings 15:15

njama aliyoifanya

"njama" "mpango." Inaweza kuelezwa wazi hii njama ilikuwa nini. "alipangaje kumuua Mfalme Zekaria" na jinsi gani alimuua Mfalme Zekaria"

yameandikwa katika Kitabu cha Matukio ya Mfalme wa Israeli

"mnaweza kuyasoma katika Kitabu cha Matukio ya Wafalme wa Israeli"

Tifsa

Hili ni jina la mji. Baadhi ya matoleo yana "Tapua," ambalo ni jina la mji mwingine.

2 Kings 15:17

Katika mwaka wa thelathini na nane wa Azaria mfalme wa Yuda

mwaka wa tisa wa Azaria mfalme wa Yuda -Inaweza kuwekwa wazi kwamba huu ni mwaka wa thelathini na tisa wa utawala wake. "Katika mwaka wa 39 wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda"

yale yaliyo maovu usoni mwa Yahwe

Uso wa Yahwe unawakilisha hukumu ya Yahwe. "yale yaliyo maovu katika hukumu ya Yahwe"

Katika maisha yake yote

"maisha" inaweza kutafsiriwa pamoja na kitenzi "kuishi." "Wakati wote ambao aliishi"

hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati

Kuacha dhambi inawakilisha kukataa kuzifanya hizo dhambi. "Zekaria hakukataa kufanya dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati" au "Aliasi kama Yeroboamu mwana wa Nebati alivyoasi"

aliyekuwa ameifanya israeli kuasi

Hapa neno "Israeli" linawakilisha watu wa ufalme wa israeli. "walikuwa wamewasababisha watu wa Israeli kuasi"

2 Kings 15:19

Pulu mfalme wa Ashuru akaja juu ya nchi

Neno "Pulu mfalme wa Ashuru" inawakilisha Pulu na jeshi lake. "Pulu mfalme wa Ashuru akaja pamoja na jeshi lake juu ya nchi"

Pulu mfalme wa Ashuru

Pulu ni jina la mwanamume ambaye alikuwa mfalme wa Ashuru. Pia alikuwa anaitwa Tiglath Pilesa.

kuja juu ya nchi

Kuja juu ya nchi inawakilisha kuja kuwashambulia watu. "nchi" inarejea kwa nchi na watu wa Israeli. "kuja pamoja na jeshi kuwashambulia watu wa Israeli"

talanta elfu moja za fedha

"talenti 1000 za fedha." unaweza kubadislisha hii na kipimo cha kisasa. " kilo elfu thalathini na nne za fedha"

ili kwamba msaada wa Pulu unaweza kuwa naye

"msaada" inaweza kutafsiriwa pamoja na kitenzi "msaada." "Pulu anaweza kumsaidia"

kuimarisha utawala wa Israeli katika mkono wake

Kuwa na ufalme katika mkono wake inawakilisha kutawala ufalme. "kuimarisha utawala wake juu ya ufalme wa Israeli"

kutoza hii pesa kutoka Israeli

"kuchukua hii pesa kutoka israeli"

shekeli hamsini za fedha

Unaweza kubadilisha kwa kipimo cha kisasa. "gram mia sita za fedha"

na hakukaa huko katika nchi

"na hakukaa huko katika Israeli"

2 Kings 15:21

je yameandikwa .. Israeli?

Hili swali linatumika labda kujulisha au kukumbusha wasomaji hiyo habari kuhusu Menahemu ipo katika hiki kitabu. "yameandikwa katika Kitabu cha Matukio ya Waflme wa Israeli."

Menahemu akalala na wazee wake

Kulala inawakilisha kufa. "Menahemu alikufa kama wazee wake walivyokufa" au "kama wazee wake, Menahemu alikufa"

Pekahia

Hili ni jina la kiume.

kuwa mfalme katika mahali pake

Neno "katika mahali pake" ni sitiari inayomaansha "badala ya yeye." "kuwa mfalme badala ya menahemu"

2 Kings 15:23

Katika mwaka wa hamsini wa Azaria mfalme wa Yuda

Inaweza kuelezwa wazi kwamba huu ni mwaka wa hamsini wa utawala wake. "Katika mwaka wa 50 wa utawala wa Azaria mfalme wa Yuda"

Pekahia

Hili ni jina la kiume.

yaliyo maovu usoni mwa Yahwe

Uso wa Yahwe unawakilisha hukumu ya Yahwe.

Hakuziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati

Kuacha dhambi inawakilisha kuacha kuzifanya hizo dhambi. "Pekahia hakuacha kufanya dhambi za Yeroboamu mwana Nebati" au "kuasi kama Yeroboamu mwana wa nebati"

alisababisha israeli kuasi

Hapa neno "Israeli" inawakilisha watu wa ufalme wa israeli.

2 Kings 15:25

Peka ... Remalia

Haya ni majina yakiume.

njama dhidi yake

"mpango wa siri kumuua Pekahia"

watu hamsini

"watu 50"

Argobu ... Arie

Haya ni majina yakiume.

ngome ya nyumba ya kifalme

"sehemu ya ngome ya nyumba ya mfalme" au "sehemu salama katika nyumba ya mfalme"

akawa mfalme katika mahali pake

Neno "katika mahali pake" ni sitiari inayomaanisha "badala yake" "kuwa mfalme badala ya Pekahia"

yameandikwa katika Kitabu cha Matukio ya Wafalme wa Israeli

"mnaweza kuyasoma katika Kitabu cha Mtukio ya Wafalme wa Israeli"

2 Kings 15:27

Katika mwaka wa hamsini na mbili wa Uzia mfalme wa Yuda

mwaka wa pili wa Azaria mfalme wa Yuda - Inaweza kuelezwa wazi kwamba huu ni mwaka wa hamsini na mbili wa utawala wake. "Katika mwaka wa 52 wa uwala Azaria mfalme wa Yuda"

yaliyo maovu usoni mwa Yahwe

Uso wa Yahwe unawakilisha hukumu ya Yahwe. "yaliyo maovu katika hukumu ya Yahwe" au "kile yahwe aonacho kuwa kiovu"

Hakuaziacha dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati

Kuacha dhambi inawakilisha kuacha kufanya hizo dhambi. "Zekaria hakuacha kufanya dhambi za Yeroboamu mwana wa Nebati" au "Aliasi kama Yeroboamu mwana wa Nebati alivyo asi"

2 Kings 15:29

Katika siku za Peka mfalme wa Israeli

Inaweza kuelezwa wazi kwamba hii inarejea kwenye wakati wa utawala wa peka. "Katika siku za utawala wa Peka mfalme wa Israeli" au "Kipindi wakati ambao Peka alikuwa mfalme wa Israeli"

Tiglath Pileseri

Katika Biblia 2 Wafalme huyu mtu alikuwa akiitwa "Puli"

Iyoni ... Abel Beth Maaka ... Yanoa ... Kadeshi ... Hazori ... Gileadi ... Galilaya ... Naftali

Haya ni majina ya miji au mikoa.

Akawachukua watu kwenda Ashuru

Hapa "Yeye" inarejea kwa Tiglathi Pileseri na inamuwakilisha yeye na jeshi lake. Kuwabeba watu wa Ashuru. "Yeye na jeshi lake waliwalazimisha watu kwenda Ashuru

watu

Inaweza kuwekwa wazi hawa ni watu wa namna gani. "wata wa hayo maeneo" au "watu wa Israeli"

Hoshea ... Ela

Haya ni majina ya kiume

njama

Njama ni mpango wa siri kwa kundi kufanya madhara kwa mwingine au kitu.

Alimshambulia na kumuua

"Hoshea alimshambulia na kumuua"

akawa mfalme katika mahali pake

Neno "katika mahali pake" ni sitiari inayomaanisha "badala yake." akawa mfalme badala ya Peka"

katika mwaka wa ishirini wa Yothamu mwana wa Uzia

Inaweza kuelezwa wazi kwamba huo ni mwaka wa ishirini wa utawala wake. "Katika mwaka wa 20 wa utawala wa Yothamu mwana wa Uzia"

yameandikwa katika Kitabu cha Matukio cha Wafalme wa Israeli

"mnaweza kuyasoma katika Kitabu cha Matukio ya Wafalme wa Israeli"

2 Kings 15:32

Katik,a mwaka wa pili wa Peka mwana wa Remalia, mfalme wa Israeli

Inaweza kuelezwa wazi kwamba huu ni mwaka wa pili wa utawala wake. "Katika mwaka wa 2 wa utawala wa Peka mwana wa Remalia, mfalme wa Israeli,"

Yothamu mwana wa Azaria, mfalme wa yuda akaanza kutawala

"Yothamu mwana wa Azaria, mfalme wa Yuda akawa mfalme wa Yuda"

Alikuwa na umri wa miaka ishirini na tano ... miaka kumi na sita

umri wa miaka mitano ... miaka kumi na sita - "Alikuwa na umri wa miaka 25 ... miaka 16"

Yerusha

Hili ni jina la mwanamke.

2 Kings 15:34

yale yaliyosahihi machoni mwa Yahwe

Neno "macho" sitiari kwa uso wa Yahwe, ambaye ni sitiari kwa ajili ya hukumu ya Yahwe. "yaliyo sahihi katika hukumu ya Yahwe"

mahali pa juu hapakuwa pameondolewa

"hakuna mtu aliyepaondoa mahali pa juu" au "Yothamu hakuwa na mtu yeyote wa kupaondoa mahali pa juu"

hapakuondolewa

Kuondolewa inawakilisha kuharibiwa. "hapakuharibiwa"

Yothamu alijenga lango la juu

"Yothamu alipajenga" inawakilisha Yothamu kuwafanya watenda kazi kuijenga. "Yothamu alikuwa na watenda kazi wake wakijenga lango la juu"

je hayajaandikwa ... Yuda?

Hili swali linatumika ama kuwajulisha au kuwakumbusha wasomaji kwamba hiyo habari kuhusu Yothamu ipo katika hiki kitabu kingine. "yameandikwa katika Kitabu cha Matukio ya Wafalme wa Yuda."

2 Kings 16

2 Kings 16:1

Katika mwaka wa kumi na saba wa mfalme Peka mwana wa Remalia

Inaweza kuelezwa wazi kwamba huu ni mwaka wa kumi na saba wa utawala wake. "Katika mwaka wa 17 wa utawala wa Peka mwana wa Remalia"

Peka ... Remalia

Haya ni majina yakiume. Peka alikuwa mfalme wa Israeli.

kile kilicho sahihi katika macho ya Yahwe Mungu wake

Hili neno "machoni mwa Yahwe" ni picha kwa ajili ya uso wa Yahwe, "kile kilichokuwa sahihi katika Yahwe hukumu ya Mungu wake" au "kile Yahwe Mungu wake alichofikiria kuwa sahihi"

kama Daudi mzee wake alichokuwa amefanya

Daudi alifanya yaliyosahihi.

2 Kings 16:3

akatembea katika njia ya wafalme wa Israeli

Kutembea inawakilisha tabia na matendo. "Mfalme Ahazi alitenda kama ambavyo wafalme wa Israeli walivyotenda" au "alifanya mambo ambayo wafalme wa Israeli waliyoyafanya"

kufuatana na machukizo yafanywayo na mataifa

Hapa "kufuata" inawakilisha yale wengine wafanyayo. "kunakili mambo maovu ambayo mataifa mengine wamefanya"

mataifa

Neno "mataifa" linawakilisha watu wa mataifa mengine. Hapa inarejea kwa watu wa mataifa waliokuwa wakiishi katika hiyo nchi. "watu wa mataifa mengine"

ambayo Yahwe aliwafukuza

"Kuwafukuza" inaamanisha "kuwatoa kwa nguvu." "ambao Yahwe aliwalazimisha kuondoka"

mbele ya watu wa Israli

Watu wa hayo mataifa walikimbia kama watu wa Israeli walivyoondoka kwenye nchi. "mbele ya watu wa Israeli waliondoka kwenye nchi" au "kama watu wa Israeli walivyoondoka kwenye nchi"

mahali pa juu, juu ya milima, na chini ya kila mti mbichi

Haya ni maeneo ambapo watu wa mataifa mengine walipoabudu miungu yao ya uongo.

chini ya kila mti mbichi

Mungu aliwataka watu wake kutoa sadaka kwake katika Yerusalimu. Neno "kila" hapa ni kutia chumvi kuonyesha jinsi Mfalme Ahazi alivyodhamiria kutokumtii Mungu kwa kutoa sadaka katika mahali pengine badala yake. "chini ya miti mingi mibichi" au "chini ya miti mingine izungukayo nchi"

2 Kings 16:5

Riseni ... Peka ... Remalia

Haya ni majina ya wanaume.

wakamzunguka Ahazi

Ahazi alikuwa Yerusalemu. Hapa "Ahazi" inamuwakilisha yeye mwenyewe na watu waliokuwa katika Yerusalemu pamoja naye. "waliuzunzunguka mji pamoja na Ahazi katika huo" au "walimzunguka Ahazi na wengine katika mji pamoja naye"

akamponya Elathi kwa Shamu

Hii inawakilisha kuchukua utawala wa Elathi ili kwamba uwe milki ya watu wa Shamu. "kuchukua utawla wa mji wa Eliathi"

Eliathi

Hili ni jina la mji.

kuwapeleka watu wa Yuda nje ya Elathi

"kuwalazimisha watu wa Yuda kuondoka Elathi"

2 Kings 16:7

Tiglath Pileseri

Katika 15:19 huyu mtu alikuwa anaitwa "Puli."

mimi ni mtumishi wako na mwanao

Kuwa mtumishi na mwana inawakilisha kutii mamlaka ya mtu. "nitakutii kana kwamba nilikuwa mtumishi wako au mwana wako"

kutoka kwenye mkono wa mfalme wa Ashuru na kutoka kwenye mkono wa mfalme wa Israeli

Mkono ni picha inayowakilisha uweza. "kutoka kwenye uweza wa mfalme wa Ashuru na kutoka kwenye uweza wa mfalme wa Israeli"

ambaye aliyenishambulia

Wafalme kumteka Ahazi inawakilisha maadui wa hao wafalme kunishambulia pamoja na maadui zao"

Mfalme wa Shamu akapanda juu Damaskasi

Neno "mfalme" linawakilisha mfalme na jeshi lake. "mfalme wa Ashuru na jeshi lake walipanda juu ya Damaskasi"

kuwabeba watu wake kama hata Kiri

Kuwabeba watu wake inawakilisha kuwalazimisha kwenda mbali. "kuwafanya watu wake wafungwa na kuwalazimisha kwenda Kiri"

Kiri

Hili ni jina la mji

2 Kings 16:10

mchoro kwa ustadi wote ulikuwa umehitajika

Hii inaweza kutafsiriwa katika mfumo tendaji. "maelekezo yote jinsi ilivyohitajika kujengwa" au "maelekezo yote ambayo watenda kazi walihiji ili kuujenga"

2 Kings 16:13

Maelezo ya Jumla:

Hivi ndivyo Ahazi alifanya baada ya kurudi kutoka Damaskasi na kutembelea madhabahu mpya aliyokuwa ameagiza ijengwe.

Alitengeneza sadaka yake ya kuteketeza

"Mfalme Ahazi alitengeneza sadaka yake ya kuteketeza"

juu ya madhabahu

Hii inarejea kwa madhabahu ambayo Mfalme Ahazi aliyomwambia Uria kujenga.

Mdhabahu ya shaba iliyokuwa mbele ya Yahwe

Hii ilikuwa ambayo watu wa Israeli waliitengeneza siku za nyuma zilizopita kulingana na maelekezo ya Mungu.

Madhabahu ya shaba yaliyokuwa mbele ya Yahwe

Neno "mbele ya Yahwe" ni picha inayorejea sehemu ambayo Yahwe alionyesha utukufu wake wa nyuma. "Madhabahu ya shaba iliyokuwa mbele ya hekalu"

kutoka mbele ya hekalu ... kutoka katikati ya madhabahu yake na hekalu la Yahwe

Haya maneno mawili yanaeleza madhabahu ya shaba ilipokuwa.

2 Kings 16:15

madhabahu kubwa

Hii inarejea kwa madhabahu ambayo Ahazi alimwambia Uria kuijenga.

sadaka ya kuteketeza ya mfalme na sadaka ya unga

Wakati Ahazi aliposema "mfalme" na "vyake," alikuwa akijirejea yeye mwenyewe. "sadaka yangu ya kuteketeza na sadaka yangu ya unga"

2 Kings 16:17

vitako vinavyobebeka

Hivi vitako vilikuwa magurudumu juu yao hivyo wangeweza kuvihamisha kuzunguka. "vitako vya kuhamisha" au "mikokoteni"

pia alichukua bahari

"Bahari" lilikuwa beseni kubwa au bakuli la maji ambalo lilitengenezwa kwa shaba. "pia aliondoa bakuli kubwa"

kwa sababu ya mfalme wa Ashuru

Kwa nini walifanya hivi inaweza kuwekwa wazi. "kumfurahisha mfalme wa Ashuru"

2 Kings 16:19

je hayajaandikwa ... Yuda?

Hili swali lilitumika pengine kuwajulisha au kuwakumbusha wasomaji ambao habari kuhusu Yothamu ipo katika hiki kitabu kingine. "yaliandikwa katika Kitabu cha matukio ya Wafalme wa Yuda."

Ahazia akalala na wazee wake

Kulala inawakilisha kufa. "Ahazia akafa kama wazee wake walivyokufa" au "kama wazee wake, Ahazia alikufa"

na alizikwa pamoja nao

"na watu walimzika pamoja na wazee wake"

akawa mfalme katika mahali pake

Hili neno "katika mahali pake." "akawa mfalme badala ya Ahazi"

2 Kings 17

2 Kings 17:1

Hoshea mwana wa Elahi

Hoshea akawa mfalme wa ufalme wa kaskazini ya Israeli.

Elahi

Hili ni jina la mwanamume.

Alitawala Samaria

Samaria ilikuwa mji mkuu wa Israeli.

uovu katika uso wa Yahwe

Hakutii sheria za Yahwe kama alivyopewa na Musa. "Katika uso wa " ni mfano kwa ajili ya hukumu au maoni. "uovu kwa Yahwe"

Hoshea akawa mtumishi na kumletea kodi

Hoshea akafanya kama Mfalme wa Ashuru alivyomwamuru na kumletea pesa ili kwamba Mfalme asiiangamize Israeli.

Shalmanesa

Hili ni jina la mwanamume.

2 Kings 17:4

So

Hili ni jina la mwanamume.

mwaka kwa mwaka

"kila mwaka" (UDB)

akamfunga na kumfungia katika gereza

"kumuweka Hoshea katika gereza" (UDB)

kuizingira

kuweka majeshi kuzunguka mji kwa ajili ya kuulzimisha kujisalimisha

kuichukua Israeli kwenda Shuru

Jina "Israeli" ni mfano kwa ajili ya watu wanaoishi huko. "kuwachukua Waisraeli kwenda Ashuru" (UDB)

Hala ... Mto Habori ... Gozani

Haya ni majina ya maeneo.

Waamedi

Hili ni jina la kundi la watu.

2 Kings 17:7

Maelezo ya Jumla:

Maelezo ya kuacha mhutasari wa hukumu ya Yahwe juu ya Israeli.

Huu uhamisho

Hii inarejea kwa mateka wa Israeli na Waashuru.

mkono wa

"Mkono" ni picha ya utawala, malmlaka au nguvu. "utawala wa"

kutembea katika mazoezi

"Kutembea" ni picha ya njia au mfumo wa tabia watu hutumia katika maisha yao. "kufanya kazi"

2 Kings 17:9

Maelezo ya Jumla:

Hadithi inaendelea kufupishwa hukumu ya Yahwe juu ya Israeli.

juu ya kila mlima mrefu na chini ya kila mti wa kijani

Huu ni ueneaji kuonyesha kwamba kuabudu miungu wa uongo ilienea. "juu ya milima mirefu na chini ya miti ya kijani kila mahali"

2 Kings 17:11

Maelezo ya Umla:

Hii hadithi inaendelea kufupishwa hukumu ya Yahwe juu ya Israeli.

kufanya mambo maovu kuchochea hasira ya Yahwe

Njia ziwezekanazo kuonyesha hii: 1) "kufanya mambo mengi maovu yaliyomfanya Yahwe kuwa na hasira" (UDB) au 2) "kufanya mambo ya dhambi yaliyomfanya Yahwe kukasirika"

kuhusu zile Yahwe alizokuwa amewaambia

"kuhusu zile Yahwe alizokuwa amewaonya"

2 Kings 17:13

Maelezo ya Jumla:

Hadithi inaendelea kufupishwa huku ya Yahwe juu ya Israeli.

Yahwe alishuhudia ... kwa kila nabii

Yahwe alizungumza kupitia manabii.

Keuka kutoka njia zako mbaya

"Kuacha kufanya mambo maovu uliyokuwa ukiyafanya"

nakuletea watumishi wangu manabii

Manabii walitumwa na Yahwe kuwakumbusha watu wa sheria za Mungu na kuzitii.

2 Kings 17:14

Maelezo ya Jumla:

Muhtasari wa hukumu wa Yahwe juu ya Israeli unaendelea.

walikuwa wakaidi

Hawakuwa tayari kufuata sheria za Mungu na kumtegemea Yahwe kama Mungu wao.

walikataa maagizo yake

Walikataa kutii shiria za Yahwe.

Walifuata mambo yasiyofaa

Walifuata mambo ya watu waliowazunguka.

kutokufuatisha

"kutonakili"

2 Kings 17:16

Maelezo ya Jumla:

Muhtasari wa hukumu ya Yahwe juu ya Israeli unaenedelea.

sanamu za kusubu

Sanamu za kusubu ni vitu vilivyotengenezwa kwa kuchemsha chuma kuwa umbo (au finyanga) kutengeneza umbo.

uchawi

"uchawi" (UDB)

wakajiuza wenyewe kufanya yale ambayo yalikuwa maovu usoni pa Yahwe

"Kujiuza wenyewe" ni picha kwa ajili ya kufanya kabisa kufanya yale yaliyo maovu. "kufanya wenyewe kufanya mambo ambayo Yahwe alisema yalikuwa maovu"

kuwaondoa usoni mwake

"Uso" ni picha ya kuwa ndani uangalifu wa Yahwe hivyo hawajali tena. "kuwaondoa kutoka kwenye uangalizi wake"

2 Kings 17:19

Maelzo ya Jumla:

Mhutasari wa huku ya Yahwe unaendelea juu ya Israeli pamoja na jinsi Yuda alivyojisikia kwenye kuabudu sanamu.

Yuda

Mahali "Yuda" ni picha kwa ajili ya watu waishio huko. "watu wa Yuda"

aliwatesa

"Yahwe aliwaadibu Waisraeli"

kuwatia kwenye mkono wa wale wenye kuwateka nyara

"Mkono" ni picha ya kwa ajili ya utawala, nguvu au mamlaka. "kuwapeleka juu ya wale walio waibia mali zao"

hadi atakapokuwa amewatupa usoni mwake

"uso wake" ni picha kwa ajili ya umakini na kujali.

2 Kings 17:21

Maelezo ya Jumla:

Sabau ya hukumu ya Yahwe juu ya Israeli kuendelea kuhusiana na historia nyuma yake.

Akawatoa

"Akawatoa" ni picha ya kuwatoa kwa kikatili. "Yahwe aliwatoa watu wa Israeli"

kutoka kwenye ukoo wa kifalme wa Daudi

"kutoka kwenye uzao wa Daudi" (UDB)

akawapeleka Israeli mbali na kumfuata Yahwe

"aliwageuza watu wa Israeli mbali na kumfuata Yahwe"

hawakujiepusha nazo

"Waisraeli hawakuacha kufanya hizi dhambi" au "Hawakugeuka kutoka kwenye hizo dhambo" (UDB)

basi Yahwe akawaondoa Israeli kutoka usoni mwake

"Uso" ni picha ya umakini na kujali. "Basi Yahwe aliwaondoa watu wa Israeli kutoka kwenye uangalifu wake na utunzaji"

2 Kings 17:24

Maelezo ya Jumla:

Hukumu ya Yahwe inaendelea juu ya wenyeji wa Waashuru mpya waliozoea dini zao za kipagani.

Kuthi ... Ava ... Hamathi ... Sefarvaimu

Hizi ni sehemu katika ufalme wa Kiashuru.

Ilitokea mwanzoni mwa makazi yao huko

"Wakati hao watu walipoishi kwa mara ya kwamnza huko"

Mataifa uliyoyachukua na kuyaweka katika miji ya Samaria

"Watu uliowaondoa kutoka nchi nyingine na kuwapeleka kuishi katika miji ya Samaria"

hawakujua yale mambo waliyokuwa wanatakiwa kuyafanya kwa mungu wa nchi

"hawakujua jinsi ya kumwabudu Mungu ambaye aliyeabudiwa na Waisraeli katika hii nchi" (UDB)

2 Kings 17:27

Mchukueni mmoja wa makuhani hapo ambaye mmemleta kutoka huko

"Mchukueni mmoja wa makuhani kutoka Samaria aliyebaki huko,"

na kumruhusu awafundishe

"na kumruhusu kuhani Msamaria kuwafundisha watu wanaoishi huko sasa"

2 Kings 17:29

Sakoth Benithi ... Nergali ... Ashma ... Nibhazi ... Tartaki ... Adrameleki ... Anameleki

Haya ni majina ya miungu, wote wakiume na wakike.

Kuthahi ... Hamathi

Haya ni majina ya mahali.

Waavi ... Sefarvaimu

Haya ni majina ya makundi ya watu.

wakawachoma watoto wao katika moto

"wakawatoa dhabihu watoto wao wenyewe" (UDB) au (wakawachoma watoto wao katika moto kama dhabihu"

2 Kings 17:32

Wao

Hii inawahusu watu wapagani ambao mfalme wa Ashuru aliwahamisha kwenda miji ya Samaria.

2 Kings 17:34

wameshikilia tamaduni zao

"waliendelea katika tabia zao zile zile kama zamani."

Wala hawamwogopi Yahwe

Watu walivutiwa na kumpendeza Yahwe pekee. Wala hawakuwa na shauku wala kutokuwa makini Yahwe alikuwa na shauku katika mahusiano nao.

2 Kings 17:36

Maelezo ya Jumla:

Ufupisho unaelekea mbele mwishoni pamoja kwa muomba Yahwe pekee.

pamoja na nguvu kubwa na mkono ulionyooshwa

Neno "mkono ulionyooshwa" ni picha ya kuonyesha nguvu na kumaanisha kimsingi jambo moja kama "nguvu kubwa." pamoja na nguvu kubwa" (UDB)

kuzishika

"kuzitii"

2 Kings 17:39

Maelezo ya Jumla:

Ufupisho sasa unaishia na ombi kumwabudu Yahwe pekee na maelezo ya dhambi za watu.

Hawatasikiliza

"Sikiliza" ni picha ya kuvuta usikivu na kutenda juu ya amri. "Hawakutii"

haya mataifa yalimwogopa Yahwe

Haya mataifa yalimwogopa Yahwe pekee kuelekea kumpendeza vile vile kama walivyoitenda miungu yao.

hata leo

"Siku hi" ni picha kwa ya kipindi ambacho mwandishi alichoishi.

2 Kings 18

2 Kings 18:1

Maelezo ya Jumla:

Hezekia akawa mfalme juu ya Yuda katika sehemu ya baba yake Mfalme Ahazi.

Hoshea ... Ela ... Zekaria

Haya ni majina ya wanaume.

Abija

Hili ni jina la mwanamke.

Alifanya yale yaliyo sahihi usoni mwa Yahwe

"Katika macho" ni mfano wa umakini wa Yahwe na kujali. "Mfalme Hezekia alifanya yale yaliyokuwa sahihi mbele ya Yahwe" au "Hezekia alifanya mambo ambayo Yahwe alisema yalikuwa sahihi"

2 Kings 18:4

Maelezo ya Jumla:

Hadithi ya utawala wa Mfalme Hezekia inaendelea.

Aliziondoa mahali za juu, akaiharibu nguzo ya jiwe, akaikata hiyo nguzo ya Ashera

"Hezekia aliziondoa mahali za juu za kuabudu, akaziangusha kuwa vipande vipande mawe ya kumbukumbu, na kuzikata nguzo za miti za Ashera"

Nehushtani

"Sanamu ya Joka la shaba"

2 Kings 18:6

Maelezo ya Jumla:

Hadithi ya utawala wa Mfalme Hezekia inaendelea.

alishikamana na Yahwe

Ku "ambatana na Yahwe" ni picha ya kusema uaminifu na kuambatana. "Hezekia alikuwa mwaminifu kwa Yahwe" au "Hezekia alibaki mwaminifu kwa Yahwe"

na popote alipoenda alifanikiwa

"na popote Hezekia alipoenda alifanikiwa."

mji imara

mji wenye ukuta uliouzunguka

2 Kings 18:9

Hoshea ... Ela ... Shalmanesa

Haya ni majina ya wanaume.

2 Kings 18:11

Hala ... Mto Habori ... Gozani

Haya ni majina ya mahali.

Wamedi

Hili ni jina la kundi la watu.

Basi mfalme wa Ashuru akawachukua Israeli kwenda Ashuru

"Hivyo mfalme wa Ashuru aliliamuru jeshi lake kuwachukua Waisraeli mbali kutoka nyumba zao, na kuwafanya waishi Ashuru"

sauti ya Yahwe

"Sauti" ni picha ya ujumbe kuhusu amri ya Yahwe. "amri ya Yahwe"

2 Kings 18:13

Senakerebu

Hili ni jina la mtu.

Lakishi

Hili ni jina la mji.

mji imara

Mji wenye kuta zilizoizunguka kwa ajili ya ulinzi.

Nichukue

Haya maelezo yasadiki kwamba "mimi" inawakilisha ufalme wa Hezekia. "Chukua jeshi lako nje ya eneo langu"

Popote utakaponiweka nitavumulia

"nitakulipa popote utakaponitaka"

talanta

Hili ni jina la aina ya uzito ambao ulitumika kwa ajili ya pesa.

hazina

Hapa palikuwa mahali katika mahali ambapo pesa na vitu vya thamani vilihifadhiwa.

2 Kings 18:16

mfalme wa Ashuru akalihamasisha jeshi lake kubwa, akawatuma Tartani na Rabsarisi na amiri jeshi mkuu

Senakeribu alipeleka kundi la watu kutoka jeshi lake kwenda Yerusalemu kuonana pamoja na Mfalme Hezekia, pamoja na maafisa waitwao Tartani na Robsarisi.

Tartani ... Rabsarisi

Baadhi ya Biblia zinatafsiri haya kama majina pekee. Matoleo mengine ya Biblia yanayatafsiri kama vyeo. "Tartani ... Rabsarisi" au "kiongozi wa askari ...afisa wa mahakama"

Lakishi

Hili ni jina la mji.

mfereji wa bwawa la juu

mfeji ambapo maji yalihifadhiwa katika "bwawa la juu" ububujikao kwenda mji wa Yerusalemu

kusimama huko

"na kumsubiri mfalme Ahazi huko kuonana nao"

Eliakimu ... Hilkia ... Shebna ... Joa ... Asafu

Haya ni majina ya watu.

2 Kings 18:19

Maelezo ya Jumla:

Rabshake anaendelea kusikiliza ujumbe kutoka mfalme wa Ashuru kwa watu wa Mfalme Hezekia.

Nini chanzo cha ujasiri wako? Sasa unamtumainia nani? Nani anakupa ujasiri wa kuasi dhidi yangu?

Mfalme wa Ashuru (kupitia mjumbe wake Rabshake) hajauliza haya maswali kutafuta majibu, lakini kutaka kumfanya shaka ya Mfalme Hezekia mwenyewe na msaada wa Misri. "Usimwamini kila mtu yeyote. Ulikuwa mjinga kuasi juu yangu."

kutembelea fimbo ya mwanzi huu uliopondeka wa Misri

Mfalme wa Ashuru analinganisha Misri kutembelea fimbo, unatajia hiyo itakusaidia wakati unapoiengemea, lakini badala yake itavunjika na kukukata. "msaada dhaifu kutoka Misri"

lakini kama mtu ... na kumtoboa

huyu mnenaji anaeneza picha kwa kueleza kilichotokea mwanzi unapotumika kama msaada. "lakini kama mtu atumiapo hii kwa ajili ya msaada, atajeruhiwa"

2 Kings 18:22

Maelezo ya Jumla:

Rabshake anaendelea kueleza ujumbe kutoka kwa watu wa mfalme wa Ashuru.

si yeye ambaye mahali pa juu ... Yerusalemu

Hili swali linasadiki wasikilizaji wanajua jibu na limetumika kwa ajili ya kusisitiza.

2 Kings 18:24

Maelezo ya Jumla:

Rabshake anaendelea kusema ujumbe kutoka kwa mfalme wa Ashuru kwa watu wa Mfalme Hezekia.

Wanawezaje kumpinga hata nahodha mmoja wa watumishi walio wadogo?

Aliuliza hili swali kusisitiza kwamba jeshi la Hezekia halina rasilimali kupigana' "usingelishinda kundi la maaskari walioamriwa na afisa wake mdogo."

Je nimesafiri kwenda huko juu bila Yahwe kupapigania hapa mahali na kupaharibu?

Anauliza hili swali kusisitiza kwamba Yahwe yu nyuma ya rasilimali zake kutii amri kuiangamiza Israeli. "Yahwe mwenyewe alituambia kuja hapa na kuiangamiza hii nchi!"

2 Kings 18:26

Eliakimu ... Hilkia ... Shebna ... Joa

Haya ni majina ya wanaume

katika masikio ya watu walio juu ya ukuta

"Katika maskio" ni picha ya kuweza kusikiliza. "kwa sababu watu wamesimama juu ya ukuta wataisikia na kuogopa"

Je bwana wangu amenituma kwa bwana wako na kuwachukua kuongea haya maneno? Je hajanituma kwa hawa watu ambao wameketi kwenye ukuta, ambao watakula kinyesi chao na kunywa mkojo wao wenyewe?

Anauliza haya maswali kuwahakikishia wasomaji kujua majibu kusisitiza kusudi lao kuwaangamiza na kuwadhililisha viongozi na watu wa Yerusalemu.

2 Kings 18:28

kutoka nguvu yangu

"nguvu yangu" ni picha ya uwezo wa mfalme mwenyewe. "kutoka kwangu" au "kutoka kwenye nguvu ya jeshi langu"

huu mji hautawekwa kwenye mkono wa mfalme wa Ashuru

Yahwe hatamruhusu mfalme wa jeshi Ashuru kuuchukua huu mji"

mkono

"mkono" ni ishara ya utawala, mamlaka na nguvu.

2 Kings 18:31

Fanyeni amani pamoja nami na njooni kwangu

"Tokeni kwenye mji na jisalimisheni kwangu" (UDB) au "Fanyeni makubaliano pamoja nami kujisalimisha, na tokeni kwenye mji mje kwangu"

mzabibu wake mwenyewe ... mti wake mwenyewe wa mtini ... birika lake mwenyewe

Hivi vyanzo vya chakula na maji ni picha ya ulinzi na wingi. Hii pia ilikuwa kawaida ya kueleza hili wazo.

nchi ya nafaka na divai yetu ... mkate na mashamba ya mizabibu ... na miti ya mizaituni na asali

Huu ni mfano wa vitu vizuri na wingi kila siku.

2 Kings 18:33

Maelezo ya Jumla:

Rabshake anaendelea kueleza ujumbe kutoka kwa mfalme wa Ashuru kwa watu Mfalme Hezekia.

Je miungu yoyote ... Ashuru?

Je miungu yoyote ... Ashuru? Anazungumza hili swali kusisitiza kwa sababu wanajua majibu. "Hakuna miungu ya watu iliyowaokoa ... Ashuru."

Iko wapi miungu ya ... Arpadi?

Anauliza hili swali kwa msisitizo kwa sababu wanajua majibu. "nimeiharibu miungu ya ... Arpadi"

Hamathi ... Arpadi ... Sefarvaimu ... Hena ... Iva ... Samaria

Haya ni majina ya mahali yanayowakilisha watu wanaoishi huko.

kutoka mkono wangu

"mkono" ni picha ya utawala, nguvu, au mamlaka. "nje ya utawala wangu"

je kuna mungu aliyeiokoa nchi yake kutoka nguvu yangu."

Anauliza hili swali kwa ajili ya kusisitiza kwa sababu wanajua majibu. "Hakuna mungu aliyeiokoa yake kutoka uweza wangu."

kutoka uweza wangu

"Uweza wangu" ni picha ya mtu anayeishilia. "kutoka kwangu"

Inawezekanaje Yahwe akaiokoa Yerusalemu kutoka kwenye uwezo wangu?"

Anazungumzia hili swali kwa ajili kusisitiza kwa sababu wanalijua jibu. "Hakuna njia Yahwe anaweza kuiokoa Yerusalemu kutoka uweza wangu!"

2 Kings 18:36

Eliakimi ... Shebna ... Joa ... Asafa

Haya ni majina ya wanaume.

ambaye alikuwa juu ya nyumba ya mfalme

"aliyeisimamia nyumba ya mfalme"

mtunza kumbu kumbu

"mtunza hadithi"

kamanda mkuu

ni tafsiri ya Kiebrania; wengine wanaiona hii kama jina la mtu, "Rabshake"

2 Kings 19

2 Kings 19:1

nyumba ya Yahwe

Hii ni njia nyingine ya kusema "hekalu la Yahwe."

Eliakimu ... Shebna ... Isaya ... Amozi

Haya ni majina ya wanaume.

Alimtuma Eliakimu

"Hezekia alimtuma Eliakimu"

wote walikuwa wamefunikwa na nguo za magunia

"wote waliovaa nguo za magunia"

2 Kings 19:3

siku hii ni siku ya mateso

Hapa "siku" ni neno lenye maana sawa na mda. "Huu ni wakati wa dhiki"

wakati umewadia watoto kuzaliwa, lakini hakuna nguvu ili wazaliwe

Hii ni picha ya kuelezea jinsi watu na viongozi wao wamekuwa wadhaifu na kutoweza kupigana na adui.

maneno yote

"Maneno" ni neno lenye maana sawa na ule ujumbe wa maneno.

inua maombi yako juu

Hii ni njia ya kawaida (neno) kutumia tendo la kuinua picha ya kuwakilisha maombi kwa bidii kwa Yahwe ambaye yuko juu yetu. "omba kwa bidii"

2 Kings 19:5

nitaweka roho ndani yake, na yamkini atasikia taarifa na kurudi kwenye nchi yake mwenyewe

"Nitatawala mtazamo wa mfalme wa Ashuru, hivyo wakati asikiapo taarifa, atataka kurudi kwenye nchi yake mwenyewe"

nitaweka roho katika yeye

Hapa "roho" huenda linarejea kwa mtazamo wake na mawazo, kuliko kuliko ukiroho. "nitashawishi kufikiri kwake" au "nitamfanya kufikiria tofauti"

nitamfanya afe kwa upanga

"Kuanguka kwa upanga" ni picha ya kuuawa. "nitamfanya afe kwa upanga" au "nitawafanya watu wamuue kwa upanga"

2 Kings 19:8

kamanda mkuu

"afisa kutoka Ashuru msimamizi chini ya mfalme"

kumkuta mfalme wa Ashuru akipigana

"aligundua kwamba jeshi la Ashuru lilikuwa likipigana"

Libna ... Lakishi

Majina ya miji katika ufalme wa Yuda.

Senakeribu ... Tirhaka

Haya ni majina ya wanaume.

alihamasisha kupigana dhidi

"aliliandaa jeshi lake kupigana dhidi ya Ashuru"

hivyo akamtuma

"hivyo Senakeribu aliwatuma"

ujumbe

Huu ujumbe uliandikwa katika barua.

2 Kings 19:10

Maelezo ya Jumla:

Huu ni ujumbe ambao Mfalme Senakaribu wa Ashuru aliutuma kwa Mfalme Hezekia.

Asikudanganye Mungu wako unayemwamini, kusema

"Usimwamini Mungu wako unayemwamini. Anadanganya wakati asemapo"

mkono wa mfalme wa Ashuru

"mkono" ni picha ya utawala, mamlaka au nguvu. "utawala wa serikali ya Ashuru"

Ona, umesikia

"Tazama, umesikia" au "Yamkini umesikia" (UDB). Hapa "ona" ilitumika kuleta usikivu kwa kile alichokuwa anataka kukisema.

Kwa hiyo je utaokoka?

Senakaribu alitumia hili swali kusisitiza kwamba Mungu hataweza kuwaokoa. "Mungu wako hatakuokoa" au "Hutaweza kukimbia popote"

2 Kings 19:12

Maelezo ya Jumla:

Ujumbe wa falme Senakaribu kwa Mfalme Ahazi unaendelea.

miungu wa mataifa wamewaokoa

Hili swali linaonyesha Hezekia anajua jibu na kupatia msisitizo. "miungu wa mataifa hawakuwaokoa bila shaka"

baba zangu

"wafalme wa Ashuru aliyepita" au "majeshi yaliyopita ya wafalme wa Ashuru" (UDB)

Gozani ... Harani ... Resefu ... Edeni ... Telasar ...Hamathi ... Arpadi ... Sefarvaimu ... Hena ... Iva

Haya yote ni majina ya mahali.

2 Kings 19:14

hii barua

Hii inarejea kwa barua ambayo Mfalme senakeribu wa Ashuru aliituma kwa Hezekia.

2 Kings 19:16

Maelezo ya Jumla:

Mfalme Hezekia anaendelea kuomba kwa Yahwe baada ya kupokea barua kutoka kwa Mfalme Senakeribu wa Ashuru.

Tega sikio lako, Yahwe, na usikie. Fungua macho yako, Yahwe, na tazama

Sentensi hizi zote zinamsihi Yahwe kuvuta usikivu kwa vitu ambavyo Senakaribu anasema.

Tega sikio lako, Yahwe, na usikie

Maneno "Tega sikio lako" na "sikia" vinamaanisha kitu kimoja ni yanaongeza msisitizo kwenye maombi. "Yahwe, tafadhali sikiliza anachokisema."

Fungua macho yako, Yahwe, na ona

Maneno "Fungua macho yako" na "ona" yanamaanisha kitu kimoja na kuongeza msisitizo kwenye maombi. "Yahwe, tafadhali kuwa makini kwa kile kinachotokea."

Wameweka miungu yao kwenye moto

Wafalme wa Ashuru wamewachoma miungu ya mataifa mengine.

Waashuru wamewaangamiza

Waashuru wameiangamiza miungu yote ya mataifa na mataifa.

2 Kings 19:19

Maelezo ya Jumla:

Mfalme Hezekia anaendelea kuomba kwa Yahwe baada ya kupokea barua kutoka kwa Mfalme Senakeribu wa Ashuru.

nakusihi

"nakuomba,"

kutoka kwenye nguvu yake

"kutoka kwenye nguvu ya Mfalme wa Ashuru" (UDB) au "kutoka kwenye majeshi ya Mfalme wa Ashuru."

2 Kings 19:20

Bikira binti Sayuni

"Bikira binti Sayuni ni picha ya watu wa Yerusalemu kana kwamba ni wadogo, mahiri na mzuri. "Watu wazuri wa Yerusalemu" Neno "binti" lilitumika kumpatia mtu tabia kwenye mji na baadhi ya waandishi wa kibiblia.

Bikira binti Sayuni amekudharau na kukucheka kwa dharau. Binti wa Yerusalemu akatikisa kichwa juu yako

Sentensi hizi zote zinakusudia kutoa maana moja.

Binti wa Yerusalemu

"Binti" ni picha ya watu wa Yerusalemu. "Watu wa mji wa Yerusalemu"

akatikisa kichwa juu yako

Hili tendo ni picha ya kuwakilisha dharau kwenye kuburi cha Waashuru.

kuinua macho yako katika majivuno

Inua macho yako katika majivuno" ni ishara ya mwenyeh kiburi au kuonyesha uso wa kiburi.

Mtakatifu wa Israeli

Msemo wa Mungu wa Israeli, Yahwe.

2 Kings 19:23

Maelezo ya Jumla:

Hii inaendeleza ujumbe kutoka kwa Yahwe uliotolewa kwa Isaya, nabii, kwa Mfalme Hezekia kuhusiana na Mfalme Senakeribu.

mmemnajisi Yahwe

Ku "asi" ni kukataa kwa uwazi au dhihaka.

nimepanda ... nitaangusha chini ... nitaingia

Haya majivuno yalifanywa na Senakeribu yangeweza kukamilishwa na jeshi lake.

Nimekausha mito yote ya Misri chini ya soli ya miguu yangu

"Na kwa kutembea kupitia kijito cha Misri, tumevikausha vyote!"

2 Kings 19:25

Maelezo ya Jumla:

Hii inaendeleza ujumbe wa Yahwe, uliotolewa kwa Isaya, nabii, kwa ajili ya Mfalme Hezekia kuhusiana na Mfalme Senakeribu.

hukusikia jinsi ... zamani?

Kufanya hatua imara hili swali linasadiki msikilizaji kujua jibu. "Hakika unajua jinsi ... zamani."

miji isiyoingilika

"miji ambayo haiwezi kunyakuliwa" au "miji iliyzizunguka kuta ndefu" (UDB)

mimea katika shamba, majani ya kijani

Hii picha inalinganisha majanga dhaifu ya Ashuru mimea dhaifu kuendelea. "kama mimea dhaifu na majani katika shamba" (UDB)

majani juu kwenye dari au kwenye shamba, lililochomwa kabla halijakua

Hii inaendeleza kulinganisha picha ya waathiriwa dhaifu wa Ashuru.

2 Kings 19:27

Maelezo ya Jumla:

Hii inaendeleza ujumbe kutoka kwa Yahwe, uliotoklewa kwa Isaya, nabii, kwa Mfalme Hezekia kuhusiana na Mfalme Senekeribu.

kuyafikia masikio yangu

"hasira yako inapiga kelele kuhusu mimi,"

kwa sababu kiburi chako kimeyafikia masikio yako

"Masikio" ni picha ya kusikiliza au kusikia. "kwa sababu nimesikia maneno yako ya majivuno,"

Nitaweka kulabu yangu kwenye pua yako, na hatamu yangu kwenye mdomo wako

"Kulabu" na "hatamu" (kuongoza farasi) ni picha ya utawala kwa ajili ya Yahwe wa Senakeribu. "Nitakutawala kama mnyama."

nitakurudisha nyuma kwa njia iliyoijia

Kwamba Senakeribu atarudi nyumbani kabla hajaweza kuishinda Yerusalemu inaweza kuwekwa wazi. "Nitakufanya kurudi katika nchi yako mwenyewe kama ulivyokuja, bila kuishinda Yerusalemu."

2 Kings 19:29

Maelezo ya Jumla:

Hapa Isaya anaongea na Mfalme Hezekia. Anaendelea kutumia msambamba wowote.

viotavyo porini

"viotavyo bila kupandandwa,"

Mabaki ya nyumba ya Yuda ambayo yataokoka yatachukua tena mizizi na kuzaa matunda

"Watu wa Yuda waliosalia hai watafufuliwa uzima wao na ustawi."

Wivu wa Yahwe wa majeshi utafanya hivyo

"Tendo thabiti la Yahwe litafanya hii itokee."

2 Kings 19:32

Maelezo ya Jumla:

Huu ndio mwisho wa ujumbe kutoka kwa Yahwe, uliozungumzwa kupitia nabii Isaya kwa Mfalme Hezekia.

wala kupiga mshale hapa

"Mshale" ni picha ya kuwakilisha vifaa vyote vya kivita na uharibifu.

au kujenga boma dhidi yake

"na wala hawatajenga matuta marefu ya dunia dhidi ya ukuta kuwawezesha kuuteka mji." (UDB)

Hivi ndivyo asemavyo Yahwe

Kwa Yahwe ku "sema" ni ahadi ya Yahwe kuahidi agano au kufanya kile alichokisema atafanya.

kwa ajili yangu mwenyewe na kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu

"kwa ajili yangu mwenyewe na kwa sababu ya kile nilichokiahidi kwa Mfalme Daudi, aliyeniokoa vema." (UDB)

2 Kings 19:35

Ikawa kuhusu

"Ilitokea"

Wakati watu walipoamka

"wakati watu waliokuwa wameachwa hai walipoamka asubuhi iliyofuata"

Nisroki ... Adramaleki ... Shareza ... Esarhodani

Haya ni majina ya kiume.

2 Kings 20

2 Kings 20:1

Weka nyumba yako katika mpangilio

"Nyumba" ni picha kwa kile kilichokuwa chini ya utawala wa Hezekia. "Toa maelezo ya mwisho kwa wafanyakazi wako na serikali"

kukumbuka

Hii ni njia ya kawaida ya kuzungumza, lugha, kumsihi Yahwe kukumbuka. "kumbuka"

tembea

"tembea" ni ishara ya mwenedo wa maisha.

nzuri usoni mwako

Hapa uso unawakilisha hukumu au tathmini. "katika hukumu yako"

2 Kings 20:4

neno la Yahwe likaja

"Neno" ni picha ya ujumbe wa Yahwe uliofunuliwa kwa Isaya. Hii ni njia ya kawaida ya kuongea, lugha. "Yahwe alizungumza neno lake"

Nimesikia maombi yako, na nimeyaonamachozi yako

Sehemu ya pili inaimarisha sehemu ya kwanza kufanya ujumbe mmoja kwa kutumia usambamba. "Nimesikia maombi yako na kuona machozi yako."

siku ya tatu

"siku mbili kutoka sasa" (UDB) Siku Isaya aliposema hii ilikuwa siku ya kwanza, hivyo "siku ya tatu" ingekuwa sawa na "siku mbili kutoka sas."

2 Kings 20:6

Maelezo ya Jumla:

Ujumbe kutoka kwa Yahwe kwa Mfalme Hezekia kupitia nabii Isaya unaendelea.

Miaka kumi na tano

miaka 15

kutoka kwenye mkono wa mfalme wa Ashuru

"Mkono" ni ishara ya nguvu, mamlaka na amri. "kutoka kwa amri ya mfalme wa Ashuru"

mkate wa tini

"gundi iliyotengenezwa na tini iliyochemshwa

Walifanya hivyo na kuiweka juu ya jipu lake

"Watumishi wa Hezekia walifanya hivyo na kuweka ile gundi kwenye uvimbe wa Hezekia"

2 Kings 20:8

Je kivuli kitaenda mbele ngazi saba, au kurudi nyuma hatua saba?"

Chanzo cha kivuli kiendapo mbele hatua kumi, au kirudipo hatua kumi?"

ngazi saba

Haya maelezo yanarejea kwa Ahazi "ngazi za Ahazi" katika 20:10. Hii ilikuwa ni kama ngazi maalumu zilizojengwa kwa ajili ya Mfalme Ahazi katika njia hii kwamba ngazi zake ziliweka alama za masaa kuwa wakati jua lichomoapo kuendelea karibu nao. Kwa njia hii, ngazi zinahumu kueleza muda wakati wa mchana.

2 Kings 20:10

Ni kitu chepesi kwa kivuli kwenda mbele hatua kumi

Kwa nini "ni kitu rahisi" kinaweza kuanza wazi. "Ni rahisi kusababisha kivuli kwenda mbele hatua kumi, kwa sababu hicho ni kitu cha kawaida kufanya"

ngazi za Ahazi

Hii ilikuwa ni kama ngazi ya pekee ilijengwa kwa ajili ya Mfalme Ahazi.

2 Kings 20:12

Merodaki Baladani ... Baladani

Haya ni majina ya mfalme wa Babeli na wana wake.

zisikilize hizo barua

(1) "kwa umakini fikiria hizo barua" au 2) "sikia ujumbe kutoka kwa mfalme wa Babeli"

Hapakuwa na kitu ... ambacho Hezekia hakuwaonyesha

"Hakuna" na "hapana" kushauriana kila mmoja kufanya wazo chanya.

2 Kings 20:14

hawa watu

Hii inarejea kwa watu waliotumwa kwa Mfalme Hezekia pamoja na ujumbe na zawadi kutoka Berodaki Baladani.

Wameona kila kitu kwenye nyumba yangu. Hakuna kitu miongoni mwa vitu vyangu vya thamani ambavyo sijawaonyesha

Hezekia anatubu katika wazo hilo hilo katika njia mbili kusisitiza hatua yake.

Hakuna kitu miongoni mwa vitu vyangu vya thamani ambavyo sijawaonyesha

"Hakuna jambo" na "hakuna" shauriana wenyewe kwa wenyewe nje kufanya wazo chanya. Huu ubaguzi umetumika kwa ajili ya kusisitiza. "Nimewaonyesha hasa kila mmoja vitu vyangu vya thamani"

2 Kings 20:16

Hivyo Isaya akamwambia Hezekia

Kwa nini usemi wa Isaya unaweza kuwa wazi. "Hivyo kwa sababu Isaya alimfahamu Hezekia alivyokuwa mpumbavu kuwaonyesha watu vitu vyake vyote vya thamani, Isaya alimwambia"

neno la Yahwe

"Neno" ni picha kwa ajili ya ujumbe ambao una neno ndani yake. "ujumbe wa Yahwe"

Tazama, siku zinakaribia kuja wakati

"Nisikilize, siku yaja kutakuwa wakati"; "Tazama" imetumika kuleta umakini kwa kile Isaya anachotaka kumwambia Hezekia.

siku

"Siku" inatumika kurejea shubiri isiyoelezeka.

2 Kings 20:19

kwa kuwa alifikiri

"Kwa sababu Hezekia alifikiri"

je hakutakuwa na amani na utahbiti huko katika siku zangu?

Hezekia anauliza hili swali kwa kusisitiza kujua jibu tayari. "Ninaweza kuwa na uhakika kwamba kutakuwa na amani na thabiti katika siku zangu."

bwawa

Eneo dogo litunzalo maji

mfereji

Njia ya kubebea maji

je yameandikwa katika Kitabu cha matukio ya Wafalme wa Yuda?

Hili swali linatumika kumkumbusha msomaji haya mambo hameandikwa. "yameandikwa katika kitabu cha historia cha Wafalme wa Yuda."

2 Kings 21

2 Kings 21:1

Hefziba

Mama wa Mfalme Manase

yale yaliyo maovu usoni mwa Yahwe

"uove" "mambo ambay ... mabay." Hapa "uso" wa Yahwe unajea vile uhukumuvyo au kuamua juu ya mambo.

kama mambo ya machukizo

maana nyingine iwezekanayo ni "pamoja na mambo ya machukizo."

akaijenga tena

Manase akaijenga tena"

2 Kings 21:4

Maelezo ya Jumla:

Hadithi ya utawala wa Mfalme Manase inaendelea.

Jina langu ndipo litakuwa Yerusalemu milele

Jina ni picha kwa ajili ya mtu. "Yerusalemu ndipo nitalifanya jina langu lijulikane mimi ni nani."

akajenga madhabahu kwa ajili ya nyota zote za mbinguni katika behewa mbili za nyumba ya Yahwe

Inaonekana kwamba, alijenga haya madhabahu ili watu waweze kufanya dhabihu na kuabudu nyota. "alijenga nyota kwenye nyua mbili za nyumba mbili za Yahwe ili kwamba watu waweze kuziabudu nyota na kuzitolea dhabihu"

Alimuweka mtoto wake kwenye moto

Unaweza kuweka wazi kwa nini alimuweka mtoto wake kwenye moto na nini kilitokea baada ya kufanya hivyo. "Alimchoma mwanae kwenye oto hadi kufa kama sadaka kwa miungu wake."

kutaka shauri

"tafuta habari kutoka"

uovu usoni mwa Yahwe

"uovu" "mambo ambayo ..." Hapa "uso" wa Yahwe unarejea au kuamua juu ya thamani ya jambo.

2 Kings 21:7

Maelezo ya Jumla:

Hadithi ya utawala wa Mfalme inaendelea.

ambayo aliitengeneza

Manase ni kama hakufanya kazi. Watumishi wake walimaliza kufanya kazi. "ambayo Manase aliagiza watenda kazi wake waifanye"

ambako nitaliweka jina langu milele

"ambako nataka watu wangu waniabudu milele"

miguu ya Israeli

Miguu ni mfani wa kwenye Biblia kwa ajili ya mtu, na jina la kundi la watu ni mfano wa watu wenyewe. "Waisraeli"

hata zaidi kuliko yale ya mataifa ambayo Yahwe aliyaharibu mbele ya watu wa Israeli

Hapa "mataifa" inawarejea watu ambao waliishi katika ya "Kanaanani" kabla ya Waisraeli hawajafika. "hata zaidi ya watu ambao Yahwe aliwaangamiza kama watu wa Israeli kuendelea kwenye nchi"

2 Kings 21:10

sanamu," kwa hiyo Yahwe, Mungu wa Israeli, asema, "Tazama

Tafsiri hii inaeleweka maneno "kwa hiyo ... asema" manabii wanaotarajiwa. Maana nyingine iwezekanayo ni kwamba Yahwe anarejea kwake mwenyewe kana kwamba alikuwa mtu mwingine: "sanamu. Kwa hiyo Yahwe, Mungu wa Israli, asema, 'Tazama ... ona."

kila alisikiaye, masikio yake yote yatang'aa

Hisia halisi ni ishara kwa ajili ya mhemko wa hisiaambao unaoisababisha. "wale wasikiao kile Yahwe afanyacho, kitashtusha."

2 Kings 21:13

nitanyoosha juu ya Yerusalemu kipimo kilichotumika dhidi ya Samaria, na kuangusha msatari utakaotumika dhidi ya nyumba ya Ahabu

Maneno "kipimo cha mstari" na "kuunganisha mstari" ni picha kwa ajili ya kiwango cha Yhwe atumiacho kuwahukumu watu. "hukumu Yerusalemu kutumia kipimo kile kile ni nilichotumia wakati nilipoihumu Samaria na nyumba ya Ahabu"

juu ya Samaria

Samaria ni mji mkuu na inawakilisha watu wote wa ufalme wa Israeli"

kipimo cha mstari

ni kifaa chenye uzito mkubwa na kamba nyembamba kitutumikacho kuonyesha kama ukuta umenyooka

nyumba ya Ahabu

Hapa "nyumba" inawakilisha familia. "familia ya Ahabu"

Nitatupa

"nitakataa"

wapatia kwenye mkono wa maadui zao

"acha maadui zao wawashinde na kuchukua nchi yao"

2 Kings 21:16

Aidha

"Vile vile" au "Kwa kuongeza"

Manase akazimwaga damu nyingi za wasio na hatia

Maneno "kumwaga damu nyingi" ni picha ya ya kuua watu kwa nguvu. "Manase aliagiza maaskari wake kuwaua watu wengi wasiokuwa na hatia"

alipoijaza Yerusalemu kutoka upande huu kwenda mwingine kwa kifo

Hii mbalagha inaweka msisitizo namba kubwa ya watu Manase aliwauwa popote Yerusalemu. "kifo" kinaweza kuelezwa kama "watu waliokufa"." "kulikuwa na watu wengi waliokufa Yerusalemu kote"

yale yaliyo maovu usoni mwa Yahwe

"uovu" mambo ambayo ni mabaya. Hapa "uso" wa Yahwe unarejea ambavyo ahukumuvyo au kuamua juu ya thamani ya jambo.

hayajaandikwa ... Yuda?

Swali halina majibu na linatumika kwa ajili ya kusisitiza.

kulala na baba zake na

Hii ni lugha ya upole ya kusema ali "kufa," kama baba zake walivyo lala, na"

bustani ya Uza

Maana ziwezekanazo 1) "bustani ambayo ilyokuwa ikimilikiwa na mtu aitwaye Uza" au 2) "Bustani ya Uza."

Amoni

Hili ni jina la mwanamume

2 Kings 21:19

Amoni ... Haruzi

Haya ni majina ya wanaume.

Meshlemethi;

Hili ni jina la mwanamke.

Yotba

Hili ni jina la mji.

yaliyo maovu usoni mwa Yahwe

"uovu" "mambo ambayo ... uovu." Hapa "uso" wa Yahwe unarejea vile ahukumuvyo au kuamua juu ya uthamani wa jambo.

2 Kings 21:21

kufuata njia zote ambazo baba yake alienenda kwazo

"kutembea katika njia zote ambazo baba yake alienenda kwazo." Jinsi ambavyo mtu aishivyo inzungumziwa kana kwamba huyo mtu alikuwa akitembea kwenye njia. "kuishi hasa ambavyo baba yake alivyoishi"

Alijitenga na Yahwe

"Alienda mbali na Yahwe" au "Hakumsikiliza tena Yahwe"

kufanya njama juu yake

"kufanya mpango na kufanya kazi pamoja kwa ajili ya kumdhuru"

2 Kings 21:24

watu wanchi

Huu ni ujumla. "baadhi ya watu wa Yuda"

njama dhidi

"kufanya mipango na kufanya kazi pamoja kudhuru"

hayajaandikwa ... Yuda?

Hili swali halina majibu na linatumika kusisitiza. "Yameandikwa ... Yuda"

bustani ya Uza

Maana ziwezekanazo ni 1) "bustani ambayo ilimilikiwa na mtu aitwaye Uza" au 2) Bustani ta Uza.

2 Kings 22

2 Kings 22:1

miaka thelathini na moja

mwaka mmoja - "miaka 31"

Yedida

Hili ni jinala mwanamke.

Adaye

Hili ni jina na mwanamume.

Bozkathi

Hili ni jina la mji wa Yuda.

Alifanya yale yaliyo sawa usoni kwenye macho ya Yahwe

Hapa "macho" inawakilisha mawazo ya Yahwe au kile anachokiwaza kuhusu jambo. "Alifanya ambacho Yahwe alikiona ni sawa" au "Alifanya kile kilichokuwa sawa kutokana na Yahwe"

Alienenda katika njia zote za Daudi baba yake

"Alitembea katika njia zote za Daudi baba yake" Yosia alitenda kama Daudi alivyofanya anazungumzia kana kwamba alitembea kwenye njia moja au kama njia ya Daudi. "Alifuata mfano wa Daudi baba yake"

hakugeuka wala upande wa kulia au kushoto

Kumtii Yahwe kikamilifu kunazungumziwa kana kwamba mtu alikuwa kwenye barabara sahihi na hakurudi kutoka kwayo. "hakufanya chochote ambacho hakikumpendeza Yahwe"

2 Kings 22:3

Ikawa kwamba

Baada ya hayo kutokea

mwaka wa kumi na nane

"kumi na nane" ni mpango wa namba ya 18. "mwaka wa 18"

Shafani ... Azia ... Meshulamu ... Hilkia

Haya ni majina ya kiume.

nyumba ya Yahwe ... katika hekalu

Hapa "nyumba ya Yahwe" na "hekalu" inamaanisha jambo moja.

Panda juu kwa Hilkia

Kirai "Panda juu" imetumika kwa sababu hekalu la Yahwe lilikuwa juu kwenye mwinuko kisha Mfalme Yosia alipokuwa. "Panda juu kwa Hilkia"

ambazo walinzi wa hekalu wamezikusanya kutoka kwa watu

"wale walinzi wa hekalu waliokuwa wamekusanya pesa kutoka kwa watu waliokuwa wamezileta kwenye hekalu la Yahwe"

Acha zigawanywe kwa mkono ya watendakzi

Hapa "mkono" inawakilisha watenda kazi wote. "Mwambie Hilkia awapatie pesa kwa watenda kazi"

2 Kings 22:6

Maelezo ya Jumla:

Ujumbe kutoka kwa Mfalme Yosia kwa Hilkia, kuhani mkuu, anaendelea.

Waacheni wapewe pesa ... walipewa ... kwa sababu waliimudu

Hapa "wao" na "-wa" inarejea kwa wafanyakazi ambao ni wasimamizi wa nyumba ya Yahwe katika 22:3.

mafundi seremala, wajenzi, na waashi

Hawa ni sawa na wafanyakazi waliopo katika nyumba ya Yahwe katika 22:3. Hapa wafanya kazi wanaelezwa kinaganaga zaidi.

wajenzi

watenda kazi wajengao kwa mbao

waashi

watenda kazi wajengao kwa mawe

zile pesa hazikutakiwa kuhesabiwa wakati walipokuwa wanapewa

"watenda kazi waliokuwa wasimamizi hawakutoa taarifa jinsi walivyotumia pesa ambayo walinzi wa hekalu waliwapatia"

kwa sababu walizimudu kwa uaminifu

"kwa sababu walitumia pesa kwa unyoofu"

2 Kings 22:8

Hilkia

Hili ni jina la mwanamume.

Kitabu cha sheria

Sheria zipendwazo sana ziliandikwa kwenye hati ya kukunja kuliko kwenye kitabu.

zilitolewa kwenye mkono wa wafanyakazi

Hapa "mkono" unawakilisha wafanyakazi kama wote.

2 Kings 22:11

Ikawa kwamba

Kama lugha yako ina njia ya kuweka alama mwanzoni mwa sehemu mpya ya hadithi, fikiria kuitumia hapa.

aliposikia maneno ya sheria

Hapa "maneno" huwakilisha ujumbe wa sheria. "alisikia sheria iliyokuwa imeandikwa katika kitabu" au alisikia sheria iliyokuwa imeandikwa katika hati ya kukunja"

alirarua mavazi yake

Hii ni alama inayoashiria huzuni kubwa sana au masikitiko.

Ahikamu ... Shafani ... Akbori ... Mikaya ... Asaya

Haya ni majina ya wanaume.

kujadiliana na Yahwe

Imewekwa wazi katika 22:14 kwamba watu wangeweza kujadiliana na Yahwe kubainisha mapenzi yake.

mjadala

kwenda kwa mtu kutafuta ushauri

maneno ya hiki kitabu yaliyopatikana

Hapa "maneno" yanawakilisha sheria. "sheria katika hiki kitabu ambacho hilikia amekikuta"

Kwa kuwa hasira kubwa ya Yahwe ambayo ametukasirikia dhidi yetu

Hasira ya Yahwe inazungumziwa kana kwamba ulikuwa mto uliokuwa unawaka. "Kwa kuwa Yahwe anahasira sana na sisi"

yote yaliandikwa kuhusiana na sisi

Hii inarejea kwenye sheria iliyokuwa imetolewa na Israeli. "yote ambayo Musa aliyoyaandika katika sheria ambayo tunatakiwa kuyafanya" au "sheria yote ya Mungu aliyoitoa kupitia Musa kwa watu wa Israeli"

2 Kings 22:14

Hulda

Hili ni jina la mwanamke.

Shalumu ... Tikva ... Harhasi

Haya ni majina ya wanaume.

mtunza kabati la nguo

Maana ziwezekanazo 1) mtu anayeangalia nguo ambazo makuhani huvaa katika hekalu au 2) mtu anayeangali nguo za mfalme.

aliishi Yerusalemu katika mtaa wa pili

Hapa "theluthi ya pili" inarejea kwa sehemu mpya ambayo ilikuwa imejengwa kwa upande wa kaskazini mwa Yerusalemu. Pia, "aliishi Yerusalemu katika sehemu mpya ya Yerusalemu"

huyo mtu aliyekutuma kwangu

Hapa "huyo mtu" inamrejea mfalme Yosia.

Nitaleta msiba mahali pake na kwa wenyeji wake

Yahwe anafanya mambo mabaya yatokee imezungumzwa kana kwamba "msiba" ulikuwa kitu ambacho angekileta hiyo sehemu.

hapa mahali

Hapa inarejea kwenye mji wa Yerusalemu ambao unawakilisha nchi yote ya Yuda.

2 Kings 22:17

Maelezo ya Jumba:

Ujumbe wa Yahwe ulitumwa kwa Mfalme Yosia kupitia Hulda, unabii, unaendelea.

hasira yangu ilikuwa inawaka dhidi ya hii sehemu, na haitazimika

Yahwe anapatwa na hasira kali sana inazungumzwa kana kwamba hasira yake ilikuwa moto uliokuwa umewaka na usiweza kuzimwa. "hasira yangu juu ya hii sehemu ni kama moto ambao hauwezi kuzimwa"

hi sehemu

Hapa "mahali" inawakilisha watu waishio katika Yerusalemu na Yuda. "hawa watu"

Kuhusu maneno uliyosikia

Hapa "maneno" inawakilisha ujumbe ambao Hulda alioungea. "kuhusu ujumbe ambao uliousikia"

Kwa sababu moyo wako ulikuwa mlaini

Hapa "moyo" unawakilisha utu wa mtu wa ndani. Kuomba samahani inazungumziwa kana kwamba moyo ulikuwa malaini. "kwa sababu ulisamehe" au "kwa sababu umetubu"

kwamba wanaweza kuwa wakiwa na laana

"ukiwa" na "laana" unaweza kuanza kama kuvumishi na kitenzi. "kwamba nitawalaani na kulaani nchi yao kuwa ukiwa"

chana mavazi yako

Hii ni tendo la ishara linaloonyesha huzuni kubwa sana masikitiko.

huu ni usemi wa Yahwe

Hapa anajizungumzia mwenyewe katika nafsi ya tatu. Inaweza kuanza katika nafsi ya kwanza. "hivi ndivyo nisemavyo"

2 Kings 22:20

Maelezo ya Jumala:

Huu ni mwisho wa ujumbe kutoka kwa Yahwe kwa mfalme Yosia kupitia utabiri wa Hulda.

Tazama, nitakukusanya na babu zako; nawe utawekwa kaburini kwako kwa amani

Sentensi zote kimsingi zinamaanisha kitu kimoja. Ni za njia ya heshima ya kusema atakufa. "Sikiliza, nikuruhusu ufe kwa amani"

Macho yako hayataona

Hapa "macho" yanawakilisha utu wote, na, "hutaona" inawakilisha hayatapitia"

janga nitakalolileta juu ya hii sehemu

Yahwe huleta mambo mabaya yatokee yazungumzwa kana kwamba "janga" yalikuwa kitu ambacho Yahwe angeleta mahali. "nitafanya mambo mabaya yatokee katika hii sehemu"

2 Kings 23

2 Kings 23:1

watu wote wa Yuda na wenyeji wote wa Yerusalemu

Hiki ni kizazi. "watu wengine wengi"

kuanzia ndogo hadi kubwa

"kutoka kwenye orodha ya chini muhimu hata kwenye orodha ya juu muhimu"

Kisha akasoma kwa sauti

"Kisha mfalme akasoma kwa saujti ili kwamba waweze kusikia"

ambalo limepatikana

"ambalo Hilkia alilipata" au "walilipata"

2 Kings 23:3

tembea na Yahwe

Vile mtu aishivyo inaongea kana kwamba huyo mtu alikuwa akitembea kwenye njia, "kutembea naye" mtu mmoja ni ishara kwa kufanya ambacho huyo mtu mwingine kufanya au kutaka wengine kufanya. "ishi kumtii Yahwe"

amri zake, maagizo yake, na sheria zake

Haya maneno yote yanamaanisha maana moja. Kwa pamoja yasisitiza kila kitu ambacho Yahwe alichoamuru katika sheria.

kwa moyo wake wote na roho yake

Lugha "kwa moyo wake wote" inamaana "kabisa" na "kwa roho yake yote" inamaana "pamoja na uhai wake wote" au "kwa nguvu zake zote"

ambayo yaliandikwa kkatika hiki kitabu

"ambayo yaliandikwa katika hiki kitabu" au "yale yaliyomo ndani ya hiki kitabu"

simama kwa agano

Hii lugha inamaanisha "kutii maneno ya agano."

2 Kings 23:4

kuhani chini yake

"makuhani wengine waliomtumikia"

mlinzi wa lango

watu ambao walikuwa wakilinda malango kwenye hekalu

kwa ajili ya Baali ... kwa nyota zote

"hivyo watu wangewatumia kumwabudu Baali ... hivyo watu wangeweza kuwatumia kuziabudu nyota zote"

Akachoma ... na kubeba ... Akawaondoa

Mifano miwili ya "Yeye" inamrejea Yosia, lakini inaweza kuwa bora kutafsiri ili kwamba msomaji aelewe kwamba watu wengine, huenda Hilkia na "makuhani chini yake" (23:4), inaweza kuwa Yosia hufanya hivo.

Bonde la Kidroni ... Betheli

majina ya mahali

kwa Baali, kwa juana kwa mwezi, kwa sayari, na kwa nyota zote

"kama njia ya kumwabudu Baali, jua na mwezi, sayari, na nyota"

2 Kings 23:6

Maelzo ya Jumla

Hii inaendelea kueleza kile ambacho mflme Yosia alichokifanya katika kujibu ujumbe kutoka kwa Yahwe.

Akaiondoa ... na kuichoma ... Akaipiga ... na kuitupa ... Akavisafisha

Mifano yote ya "Yeye" inamrejea Yosia, lakini inaweza kuwa bora kutafsiri ili kwamba msomaji awaelewe hao watu wengine, huenda Hilkia na "makuhani chini yake" (23:4), yawezekana wamemsaidia Yosia kwa haya mambo.

kushona nguo

"tengeza nguo"

2 Kings 23:8

Yosia akawaleta ... na kupanajisi ... akapaharibu

Inaweza kuwa tafsiri bora ili kwamba msomaji aelewe kwamba watu wengine, huenda Hilkia na "makuhani chini yake" wanaweza kumsaidia Yosia kufanya hivi.

Geba ... Bersheba

majina ya mahali

Yoshua (liwali wa mji)

"mji wa utawala uitwao Yoshua" au kiongozi wa mji aitwaye Yoshua." Huyu ni tofauti na Yoshua kutoka katika kitabu cha Agano la Kale cha Yoshua.

ndugu zao

Hapa "ndugu" inarejea kwa makuhani wenzao aliohudumu katika hekalu.

2 Kings 23:10

Tofeli ... Ben Hinomi

majina ya mahali

akamuweka mwanaye au binti yake kwenye moto kama sadaka ya Molaki

"kumuweka mwanaye au bintiye katika moto na kuwachoma kama sadaka kwa Molaki"

Akachukua

Inaweza kuwa njia bora kutafsiri ili kwamba msomaji aelewe kwamba watu wengine, huenda Hilkia na "makuhani chini yake," wanaweza kumsaidia Yosia kufanya hivyo.

farasi

Maana ziwezekanazo ni 1) farasi halisi 2) sanamu za farasi.

alitoa kwa jua

"alitumika kuabudu jua."

Nathani Meleki

jina la kiume

2 Kings 23:12

Yosia mfalme akayaharibu ... piga ... tupa ... vunja ... katalia chini ... jaza

Inaweza kuwa tafsiri bora ili kwamba msomaji awaelewe hao watu wengine, huenda Hilkia na "makuhani chini yake"

bonde la Kidroni

jina la mahali.

hizo sehemu zikajazwa kwa mifupa ya wanadamu

"ardhi kufunikwa na mifupa ya wanadamu ili watu wasiweze kuitumia tena kama madhabahu"

2 Kings 23:15

Yosia pia akaiteketeza kabisa ... Pia alichoma ... na kupiga ... pia alichoma

Inaweza kuwa tafsiri bora ili kwamba msomaji aelewe kwamba watu wengine, huenda Hilkia na "makuhani chini yake"

aliyekuwa ameongea haya mambo kabla

"alisema hayo mambo yatatokea"

2 Kings 23:17

ukumbusho

alama au sheria ambayo humuheshimu mwanadamu.

Hivyo wakaiacha mifupa yake, pamoja na mifupa ya

"Hivyo hawakuigusa mifupa yake au mifupa ya"

2 Kings 23:19

Yosia akahamisha ... alifanya ... alichinja ... alichoma

Inaweza kuwa bora kutafsiri ili msomaji aelewe kwamba watu wengine, huenda Hilkia na "makuhani chini yake" (23:4), ingewezekana Yosia kusaidiwa kufanya haya mambo.

nini kilifanyika

"alifanya nini"

alichoma mifupa ya binadamu juu yao

"alichoma mifupa juu yao hivyo hakuna hata mmoja wao ataitumia tena"

2 Kings 23:21

Itunzeni pasaka

"Lazima kuisherekea pasaka"

Pasakakama hiyo haijawahi kufanyika tangu siku za

"Uzao wa Israeli haukusherekea sikukuu ya pasaka kwa njia hiyo kubwa katika wakati wa"

alitawala Israeli

Jina "Israeli" linasimama kwa ajili ya uzao wa Israeli."

siku za wafalme wa Israeli au Yuda

"kipindi wakati wana wa Israeli walipokuwa na mfalme wao wa watu wa Yuda walipokuwa na mfalme wao"

Pasaka hii ya Yahwe ilisherekewa

"watu wa Yuda walisherekea hii Pasaka ya Yahwe"

2 Kings 23:24

aliwafukuza ... roho

"kuzilazimisha hizo ... roho kuishi" au "kufanya sheria ambayo wale .. roho zilizokuwa ziondoke"

wale walioongea na wafu au na roho

Maneno yafananayo, "wale wliouawa na wafu na ... wale waliouawa na roho."

miungu

vitu ambavyo watu huamini kimakosa vyenye nguvu ya ajabu

ambaye amemgeukia Yahwe

"alijitoa mwenyewe kabisa kwa Yahwe"

Hapakuwa na mfalme kama Yosia aliyeinuka baada ya yeye

"Na tangu hapo hajawahi kutokea mfalme kama Yosia"

2 Kings 23:26

Walakini

Mwandishi anatumia hili neno kuonyesha kwamba hata kama haya mambo yote ambayo Yosia aliyafanya yalikuwa mema, Yahwe bado alikuwa na hasira na Yuda.

Yahwe hakugeuka kutoka kwenye ukali wa hasira yake, ambayo ilikuwa dhidi ya

Moto ni ishara ya hasira, na moto ni ishara ya hasira kuanza kuwa na hasira. "ukali" na "hasira" inaweza kuatafsiriwa kama vivumishi. "Yahwe hakugeuka kutoka kwenye ukali wa hasira yake kubwa, ambayo ilikuwa juu ya" au "Yahwe hakuacha kuwa mkali kwa sababu alikuwa na hasira na"

aligadhabisha

"alisababisha kuwa na hasira"

kuondoa usoni kwangu

"kutoka nilipo" au "kutoka kuwa karibu nami"

Jina langu litakuwa huko

Jina ni badala ya heshima ambayo watu wanayotakiwa kutoa kwa mtu. "Watu watatakiwa kuniheshimu hulo"

2 Kings 23:28

hayajaandikwa ... Yuda?

Swali halina majibu na linatumika kwa ajili ya kusisitiza. "huwezi kuyakuta ... Yuda."

Katika siku zake, Farao Niko, mfalme wa Misri

"Katika kipindi Yosia alipokuwa mfalme wa Misri, Farao Niko"

Niko ... Megido

Niko ni jina la kiume. Megido ni jina la mji.

2 Kings 23:31

umri wa miaka ishirini na tatu

umri wa miaka mitatu - "umri wa miaka 23"

Hamathi

Hili ni jina la mwanamume.

Libna ... Libna ... Hamathi

Haya ni majina ya maeneo.

Yehoahazi alifanya yaliyo maovu usoni kwa Yahwe

"Uovu" unaweza kutafsiriwa kama "vitu ambavyo ... viovu." Hapa "uso" wa Yahwe unarejea vile ahukumuvyo.

kumuweka kifungoni

Baada ya kumfunga kwa minyororo, huenda alimuweka katika gereza. "kumuweka katika kifungo"

kuitoza Yuda

"kuwalzimisha watu wa Yuda kumpatia" (UDB)

talanta mia moja ... talanta moja

Talanta moja ilikuwa kama kilogramu 33. "3,3000 kilogramu ... kilogramu 33"

2 Kings 23:34

Yehoyakimu akaitoza nchi kodi

"Yehoyakimu alikusanya kodi kutoka wamilikio nchi"

watu wa nchi

"watu wa nchi ya Yuda." Maana ziwezekanazo 1) "watu walioishi katika nchi ya Yuda" au 2) "tajiri na hodari zaidi wa wale walioishi katika Yuda."

2 Kings 23:36

Zabida

Jina la kika

Pedaia

Jina la kiume

Ruma

Jina la mahali

Joakimu alifacho yaliyo maovu usoni mwa Yahwe

"uovu" unaweza kutafsiriwa kama "vitu ambavyo...uovu." Hapa "uso" wa Yahwe unarejea vile ahukumuvyo au kuamua juu ya thamani ya kitu.

2 Kings 24

2 Kings 24:1

Katika siku za Yehoyakimu

"Katika kipindi ambacho Yehoyakimu alipoitawala Yuda"

akaiteka Yuda

"aliiteka na kuishinda Yuda"

Hii ilikuwa ni kuthibitisha pamoja na neno la Yahwe ambalo aliloliongea kupitia watumishi wake manabii

"Hii ilikuwa inatokana na neno la Yahwe kwamba watumishi wake manabii walipo nena" au "Hii ilikuwa dhahiri kile Yahwe alichowaambia watumishi wake manabii kusema kitakachotokea"

2 Kings 24:3

Ilikuwa baada ya mda mfupi kwenye kinywa cha Yahwe

Baadhi ya matoleo yana, "Ilikuwa baada ya mda mfupi kwa sababu hasira ya Yahwe," ambayo ni nzuri kusoma ujumbe halisi.

kwenye kinywa cha Yahwe

Hapa "mdomo" unawakilisha amri ya Yahwe. "kama Yahwe alivyoamuru"

waondoe kwenye uso wake

"kuwaondoa" au "waharibu"

damu isiyo na hatia aliyoimwaga

Damu ni ishara kwa ajili ya uhai usio na hatia, na kumwaga damu ni ishara ya kuua watu wasio na hatia. "watu wasio na hatia aliowaua"

aliijaza Yerusalemu kwa damu isiyo na hatia

Damu ni ishara kwa uhai usio na hatia, na kumwaga damu ni ishara ya kuwaua watu wasio na hatia. "aliwaua watu wengi wasio na hatia katika Yerusalemu"

2 Kings 24:5

hayajaandikwa ...Yuda?

Hii imeandikwa kama swali lisilokuwa na majibu kwa sababu kwenye huo mda haya yalikuwa yameandikwa watu walikuwa tayari makini na hii habari.

lala na babu zake

"kufa na alizikwa karibu na babu zake"

2 Kings 24:7

Mfalme wa Misri hakushambulia tena nje ya nchi yake

"Mfalme wa Misri hakutoka kwenye nchi yake tena kuwashambulia makundi ya watu wengine"

2 Kings 24:8

Nehushta ... Elnathani

Nehushta ni jina la mwanamke. Elnathani ni jina la mwanamume.

Alifanya yaliyo maovu usoni mwa Yahwe

"uovu" unaweza kutafsiriwa kama "vitu ambavyo .. viovu." Hapa "uso" wa Yahwe unarejea ahukumuvyo au aamuavyo juu ya thamani ya kitu.

alifanya yote baba yake aliyoyafanya

Hii inajumuisha. "alifanya baadhi ya dhambi baba yake alizokuwa amezifanya"

2 Kings 24:10

Yekonia mfalme wa Yuda akatoka nje kwenda kwa mfalme wa Babeli, yeye, mama yake, maafisa wake

Unaweza kuhitaji kufanya ufafanuzi kwa nini Yekonia alienda kumlaki Nebukadreza. "Yekonia mfalme wa Yuda, mama yake, watumishi wake, wana wake, na maafisa wake wote walienda hata ambapo mfalme wa Babeli alipokuwa, kusaliti amri kwake"

Mfalme wa Babeli akamteka katika mwaka wa nane wa utawala wake

"Baada ya mfalme wa Babeli kuwa mfalme kwa mda wa miaka saba, alimchukua Yekonia"

2 Kings 24:13

Suleimani mfalme wa Israeli alivitengeneza

Unaweza kutaka kutafsiri hivi ili msomaji aelewe kwamba Suleimani anaweza kuwa alikuwa na msaada mwingine kufanya hivo.

Aliwachukua Yerusalemu wote kwenda uhamishoni

Hii ni kutengwa, na neno "Yerusalemu" ni ishara kwa ajili ya watu walioishi huku. "Nebukadreza aliwachukua watu wote muhimu kutoka Yerusalemu"

na mafundi wote, na wafua vyuma

"watu waliojua jinsi ya kufanya na kukarabati vitu ambavyo vimetengenezwa kwa chuma"

Hakuna aliyeondoka isipokuwa watu maskini kabisa katika nchi

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi chanya. "Watu maskini kabisa pekee katika nchi bado wanaishi huko"

2 Kings 24:15

elfu saba ... elfu moja

"7,000 ... 1,000"

Matania

Hili ni jina la kiume.

2 Kings 24:18

ishirini na moja ... kumi na moja

moja ... kumi na moja - "21 ... 11"

Hamutali

Hili ni jina la mwanamke.

Yeremia

Hili ni jina la kiume.

Libna

Hili ni jina la mahali

Alifanya uovu usoni mwa Yahwe

"uovu" unaweza kutafsiriwa kama "vitu ambavyo ... viovu." Hapa "uso" wa Yahwe unarejea vile ahukumuvyo au kuamua kwenye thamani ya kitu.

2 Kings 25

2 Kings 25:1

katika mwaka wa tisa

Namba tisa mara nyingi imetumika katika Biblia kueleza nafasi ya kitu kilicho katika orodha.

katika mwezi wa kumi, na siku ya kumi ya mwezi

Huu ni mwezi wa kumi wa kalenda Kiebrania. Siku ya kumi ikaribu na mwishoni mwa mwezi wa kumi na mbili kwenye kalenda za Magharibi. Hiki ni kipindi cha msimu wa baridi wakati huo huweza kuwa na baridi na barafu.

kuja na jeshi lake lote juu ya Yerusalemu

Jina "Yerusalemu" ni ishara kwa ajili ya watu waishio humu. "Kuja na jeshi lake lote kupigana juu ya watu wa Yerusalemu" au "kuja na jeshi lake lote kuishinda Yerusalemu"

siku ya tisa ya mwezi wa nne

Huu ni mwezi wa kalenda ya Kiebrania. Siku ya tisa liyo karibu na mwezi wa Saba kwa kalenda ya Magharibi. Hiki ni kipindi cha majira ya ukame wakati huo huwa na mvua kidogo au hakuna kabisa.

watu wa nchi

Hawa ni wenyeji wa Yerusalemu, pamoja na wakimbizi kutoka vijiji vilivyozunguka waliokimbia Yerusalemu wakati vita ilipoanza.

2 Kings 25:4

Kisha mji ulivunjwa kuwa

Hii inaweza kutafsiriwa katika mfumo tendaji. "Kisha jeshi la Wababeli lilivunjika kuwa mji"

watu wote wapiganaji

"mashujaa wote"

kwa njia ya lango

"kwa kutumia lango"

Wakaldayo

Baadhi ya tafsiri zinatumia "Wakaldayo" na nyingine hutumia "Wababeli." Njia zote zinarejea kwa kundi moja la watu.

Mfalme akaenda katika mwelekeo wa

"Mfalme Zakaria pia alikimbia na kuelekea mbele"

Jeshi lake lote lilitawanyika mbali naye

Hii inaweza kutafsiriwa katika mfumo tendaji. "Jeshi lake lote lilikimbia mbali naye"

2 Kings 25:6

Ribla

Hii ni sehemu ya mahali

pitisha hukumu juu yake

"amua jinsi watakavo mwadibu"

wakawachinja mbele ya macho yake

Macho yamemwona nafsi yake yote. "walimlazimisha mfalme Zedekia kuwaangalia wasiwaue wana watoto wake"

akamtoa macho yake

"Nebukadreza aliyatoa macho ya Zakaria."

2 Kings 25:8

katika mwezi wa tano, siku ya saba ya mwezi

Huu ni mwezi wa tano wa kalenda ya Kiebrania. Siku ya saba ikaribu na mwezi wa Saba kwenye kalenda ya Kaskazini.

mwaka wa kumi na tisa

Hii ni namba ya mpangilio ya namba 19.

Nebuzaradani

Hili ni jina la mtu.

Kama kwa kuta zote zilizozunguka Yerusalemu, yote

"Hivi ndivyo ilivyotokea kwa kuta zote zilizoizunguka Yerusalemu: yote"

ambaye alikuwa chini ya

"ambaye alikuwa akifuata maagizo ya"

2 Kings 25:11

Kama kwa mabaki ya watu ... mji, wale

"Hiki ni kile kilichowatokea mabaki ya watu ... mji: ambao"

mabaki ya watu waliokuwa wamebaki katika mji

"watu waliobaki katika mji"

asi kwa mfalme

"kuacha mji na kwenda kuwa na mfalme"

2 Kings 25:13

Na zile nguzo za shaba ambazo zilikuwa kwenye nyumba ya Yahwe, Wakaldayo

"Hivi ndivyo ilivyotokea kwa kwa nguzo za chuma ... Yahwe: Wakaldayo"

misimamio

Hii inarejea kwa stendi kubwa zihamishikazo pamoja magurudumu ya shaba na ekseli. "zile stendi za nguzo za kuhamisha"

bahari ya shaba

"beseni kubwa ka shaba"

zivunje kuwa vipande vipande

"kuzivunja vipande vipande" au "kuzichonga kuwa vipande vipande"

mabeleshi

Beleshi kilikuwa kifaa kilichokuwa kikitumika kusafishia madhabahu, hasa kutolea vumbi la manyoya laini ya zulia, mchanga, au majivu.

pamoja ambavyo kuhani alivyokuwa amevitunza kwenye hekalu

"ambayo makuhani walivyokuwa wakitumika katika huduma ya hekalu"

Masufuria ya kuhamishia majivu

Unaweza kuhitaji kufanya dhahiri ambapo majivu huzungumiwa. "Masufuria hutumika kwa ajili ya kutolea majivu kutoka kwenye madhabahu"

2 Kings 25:16

bahari

"beseni kubwa la shaba."

stendi

Hii inarejea kwa stendi kubwa zihamishikazo pamoja magurudumu ya shaba na ekseli. "zile stendi za nguzo za kuhamisha

dhiraa kumi na nane ... dhiraa tatu

Dhiraa ilikuwa sintimita 46. "takribani mita 8.3 ... takribani mita 1.4"

kichwa cha shaba

"msanii, mbunifu wa shaba" au kipande cha shaba pamoja na ubunifu"

kazi ya kiunzi cha fito

Huu ulikuwa ubunifu uliotengenezwa kwa tepe zilizopishana zilizokuwa zikionekana kama wavu.

vyote vilitengenezwa kwa shaba

"vilitengenezwa kwa shaba kabisa"

2 Kings 25:18

Kamanda wa mlinzi

maneno yametokea sawa sawa katika 25:8.

Seraya

Hili ni jina la mtu.

kuhani wa pili

Hili neno linamrejea Zefania. Maana nyingine iwezekanayo ni "kuhani chini ya Seraya."

walinzi wa lango

Tafsiri kama katika 7:9.

chukua mfungwa

"chukua na kutunza bila kukimbia"

afisa aliyekuwa msimamizi wa maaskari

Tafsiri nyingine inaweza kusomwa "towashi aliyekuwa msimamizi wa maaskari." Towashi ni mtu ambaye ametolewa sehemu zake za siri.

wajibu wa afisa kwa kugawa kundi la watu kwenye jeshi

Maana ziwezekanazo 1) afisa kulazimisha watu kuwa maaskari au 2) afisa kuandika chini majina ya watu watakaokuwa maaskari.

2 Kings 25:20

Nebuzaradani

Hili nina la mtu.

Ribla

Hili ni jina la mahali.

kuwaua

Hii ni njia nzuri ya kusema "wameuawa." Inaweza kuwa nzuri kutafsiri ili kwamba msomaji aelewe kwamba watu wengine wamemsaidia mfalme kufanya jivyo.

Katika njia hii, Yuda aliiacha nchi yake kwenda uhamishoni

"Hivyo Yuda alichukuliwa kutoka kwenye nchi yake kwenda uhamishoni"

Yuda aliiacha nchi yake

Yuda, jina la kundi la watu, ni kati ya watu wenyewe. Watu wa Yuda walitoka katika nchi yao"

2 Kings 25:22

Gedalia ... Ahikamu ... Shafani ... Ishmaeli ... Nathania ... Yohanani ... Karea ... Seraya ... Yezania

Haya ni majina ya wanaume.

Mnetofa

Uzao wa mtu aitwaye Netofa

Mmaaka

kutoka sehemu iitwayo Maaka

2 Kings 25:25

Mwezi wa saba

Huu ni mwezi wa saba kwenye kalenda ya Kiebrania. Iko katika kipindi cha sehemu ya mwishoni mwa Mwezi wa tisa na sehemu ya kwanza ya Mwezi wa kumi huko magharibi.

Elishama

Hili ni jina la mtu

watu wote

Hiki ni kizazi. "watu wengi"

kutoka chini kwenda juu

Hii inamaanisha "Kila mtu," ambayo ni ujumla. "kutoka chini muhimu kwenda juu muhimu" au "kila mmoja"

2 Kings 25:27

katika mwaka wa saba

mwaka wa saba

katika mwezi wa kumi na mbili, siku ya ishirini na saba ya mwezi

siku ya saba ya mwezi - Huuulikuwa mwezi wa kumi na moja wa kalenda Kiebrania. Siku ya saba ikaribu na mwanzoni mwa Mwezi wa nne kwenye kalenda kaskazini.

Evil-Merodaki

Merodaki - Hili ndivyo ambavyo jina la mtu linatamkika, namna yake.

2 Kings 25:28

kiti kizuri zaidi kuliko kile cha wafalme

Kutoa sehemu nzuri kwenye meza ya chakula ni namna ya kumheshimu. "heshima zaidi kuliko wafalme wengine"

akamvua Yekonia nguo za gerezani

Msomaji aelewe kwamba kumvua nguo zake za gerezani ni ishara ya kumfanya mtu huru.

kwenye meza ya mfalme

"pamoja na mfalme na maafisa wake"

Chakula cha siku zote kiliruhusiwa apewe yeye

Hii inaweza kufsiriwa katika umbo tendaji. "Mfalme alihakikisha kwamba alikuwa na chakula cha marupurupu siku zote"

Chakula cha kila siku kiliruhusiwa

"Pesa ya kununulia chakula"

1 Chronicles 1

1 Chronicles 1:1

Wana wa Nuhu walikuwa ni Shemu, Hamu, na Yafethi

Tafsiri zingine, pamoja na ULB na UDB, za usisha "Wana wana" ili kuweka wazi kuwa Shemu, Hamu, na Yafethi walikuwa ni ndugu na wana wa Nuhu. Lasihivyo, msomaji ata dhani kila mtu aliwakilisha kizazi kimoja mbali na Nuhu, babu yao.

Enoshi, Kenani, Mahalaleli, Yaredi ... Methusela

Haya majina ni orodha ya mababu.

1 Chronicles 1:5

Gomeri ... Dodanimu

Tafsiri haya majina jinsi ungetafsiri majina kwenye lugha yako. Haya yote ni majina ya wanaume.

Dodanimu

Hili jina uwa latafsiriwa "Rodanimu" kama kwenye UDB.

1 Chronicles 1:8

Mizraimu ... Nimrodi

Haya ni majina ya watu.

1 Chronicles 1:11

kwa yeye ambaye Wafilisti walitoka

"mababu wa Wafilisti"

1 Chronicles 1:13

Hethi

Hili ni jina la mtu.

Mwarki ... Mhamathi

Haya ni majina ya vikundi vya watu

1 Chronicles 1:17

Arfaksadi ... Yoktani

Haya ni majina ya watu.

1 Chronicles 1:20

Yoktani ... Yobabu

Haya ni majina ya watu.

1 Chronicles 1:24

Shemu ... Serugi

Haya ni majina ya watu.

1 Chronicles 1:28

Nebayothi ... Kedema

Haya ni majina ya watu.

1 Chronicles 1:32

Ketura ... Elda

Haya ni majina ya watu.

1 Chronicles 1:34

Elifazi ... Miza

Haya ni majina ya watu.

1 Chronicles 1:38

Lotani ... Ana

Haya ni majina ya watu.

1 Chronicles 1:41

Ana ... Arani

Haya ni majina ya watu.

1 Chronicles 1:43

Bela ... Beori ... Yobabu .. Zera .. Hushamu

Haya ni majina ya watu.

Dinhaba ... Bozra

Haya ni majina ya sehemu

Hushamu wa nchi ya Watemani akatawala badala yake

'Hushamu, kutoka nchi ambayo uzao wa Temani waishi, alitawala baada yake."

Watemani

Hili ni jina la kundi la watu

1 Chronicles 1:46

Hushamu ... Hadadi ... Bedadi ... Samla ... Shauli

Haya ni majina ya watu.

Avithi ... Masreka ... Rehobothi

Haya ni majina ya sehemu

1 Chronicles 1:49

Shauli ... Baali Hanani ... Akbori ... Hadari ... Mehetabeli ... Matredi ... Me Zahabu

Haya ni majina ya watu.

Pai

Hili ni jina la sehemu.

1 Chronicles 2

1 Chronicles 2:1

Rubeni ... Asheri

Haya ni majina ya watu.

1 Chronicles 2:3

Yahweh

Hili ni jina la Mungu alilo lirihidhisha kwa watu wake wa Agano la Kale.

alimzalia Peresi na Zera

"aliza wana wake Perezi na Zera"

wana wa tano

"wana wa 5"

macho ya Yahweh

"kwa mujibu wa Yahweh|"

Yahweh akamwua

Hii inamaanisha Yahweh aliruhusu Eri auliwe.

mkwe wake

Hii ina maana ya mke wa mwanae.

1 Chronicles 2:13

wa pili ... wa tatu

"mwanae wa pili ... mwanae wa tatu"

1 Chronicles 2:16

Yetheri Mwishmaeli

Hii ina maanisha kuwa Yetheri alikuwa uzao wa Ishmaeli.

1 Chronicles 2:18

aliye mzalia

"alimzaa"

1 Chronicles 2:21

aliye mzalia

"alimzaa"

1 Chronicles 2:23

aliye mzalia

"alimzaa"

1 Chronicles 2:25

Atara

Hili ni jina la mwanamke.

1 Chronicles 2:34

aliye mzalia

"alimzaa"

1 Chronicles 2:42

Wana wa Kalebu ... Maresha

Tafsri tofauti zinaelewa mahusiano miongoni mwa hawa watu kwa njia tofauti. Baadhi ya wafasiri wanaamini kwamba "baba wa Hebroni ... baba wa Rahama, baba wa Yorkeamu ... baba wa Shamai" ya maanisha "mzinduzi wa ukoo wa Hebroni," nk. Baadhi ya tafsiri za weza tumia hii lugha.

1 Chronicles 2:48

alimzaa

"alimzalia"

1 Chronicles 2:52

Wanuthi ... Waithri, Waputhi, Washumathi, na Wamishrai. Wazora na Waeshtaoli

Haya ni majina ya koo.

1 Chronicles 2:54

Wanetofathi, Atroth-Beth-Yoabu, na nusu ya Wamenuhothi na Wazori ... Watirathi, Washimeathi, na Wasukathi ... Wakeni ... Warekabu

Haya ni majina ya koo.

1 Chronicles 3

1 Chronicles 3:1

Daudi

Daudi alikuwa mwana wa Yese, aliye kuwa uzao wa Yuda.

Ahinoamu ... Abigail ... Maaka ... Hagithi ... Abitali ... Egla

Haya ni majina ya wanawake.

Talmai ... Shefatia ... Ithraeamu

Haya ni majina ya wanaume.

Danieli

Huyu mtu ana jina kama la nabii wa Israeli lakini ni mtu tofauti.

Egla mkewe

"Egla, mke wa Daudi." Daudi alikuwa na zaidi ya mke mmoja. "Mke wa Daudi Egla"

1 Chronicles 3:4

alipo tawala miaka saba na miezi sita

Hii ya weza tafsiriwa kama sentensi yenyewe: "Daudi alitawala huko miaka saba na miezi mitatu."

miaka thelathini na mitatu

miaka mitatu - " miaka 33"

Ammieli ... Shammua ... Shobabu ... Nadhani

Haya ni majina ya watu.

1 Chronicles 3:6

Ibhari ... Elishama ... Elifeleti ... Noga ... Nefegi ... Yafia ... Eliada

Haya ni majina ya wanaume.

Elishama ... Elifeleti

Haya majina yametumika kwa wana wawili.

1 Chronicles 3:10

Maelezo ya jumla:

Huu ni mwanzo wa orodha ya uzao wa Daudi ya walio kuwa wafalme.

Mwana wa Sulemani alikuwa ni Rehoboamu. Mwana wa Rehoboamu alikuwa Abiya

Sulemani alikuwa na zaidi ya mwana mmoja. Hii ni kweli kwa kwa wanaume wengine kwenye orodha. "Sulemani alikuwa baba wa Rehoboamu. Rehoboamu alikuwa baba wa Abiya"

Azaria

Hili ni jina lingine la Uzia, jina linalo julikana vizuri kwa huyu mfalme. Wafasiri wanaweza amua kutumia "Uzia" kila sehemu kwa huyu mfalme.

1 Chronicles 3:13

Maelezo ya Jumla

Huu ni mwendelezo wa orodha ya uzao wa Daudi ya walio kuwa wafalme. Tunga hizi sentensi kama ulivyo fanya kuanzia 3:10.

Amoni

Hili ni jina la mwanaume.

1 Chronicles 3:15

Maelezo ya Jumla

Huu ni mwendelezo wa orodha ya uzao wa Daudi ya walio kuwa wafalme. Tunga hizi sentensi kama ulivyo fanya kuanzia 3:10.

Yohanani ... Shalumu ... Yehoyakini

Haya ni majina ya wanaume.

1 Chronicles 3:17

Yehoyakini

Baadhi ya tafsiri zina "Yekonia," ambayo ni mbadala wa "Yehoyakini."

watekwa

Hii inaweza kuwa cheo kilichopewa Yehoyakini kwasababu alichukuliwa matekani. Ingawa, baadhi ya tafsiri za eleza hilo neno kama "Asiri," jina la mmoja wa wanae.

YehoYakini ... Shealtieli, Malkiramu, Pedaya, Shenezari, Yekamia, Hoshama, na Nedabia

Haya ni majina ya wanaume.

1 Chronicles 3:19

Pedaya ... Shimei ... Meshulamu ... Hanania ... Hashuba ... Oheli ... Berekia ... Hasadia ... Yushabu Hesedi ... Pelatia ... Yeshaia ... Refaya ... Arnani ... Shekania

Haya ni majina ya wanaume.

Shelomithi

Hili ni jina la mwanamke.

Obadia

Huyu mwanaume ana jina sawa na nabii wa Israeli Obadia lakini ni mtu tofauti.

uzao wake zaidi walikuwa ni Arnani, Obadia, na Shekania.

Tafsiri tofauti zinawaweka hawa watu katika mahusiano tofauti wao kwa wao, kwasababu lugha ya Kiebrania haijafafanua kuwahusu.

1 Chronicles 3:22

Shemaia ... Hatushi ... Igali ... Baria ... Nearia ... Shafati ... Elionai ... Hizekia ... Azrikamu ... Hodavia ... Eliashibu ... Pelaya ... Akubu ... Delaia ... Anani

Haya ni majina ya wanaume.

1 Chronicles 4

1 Chronicles 4:1

Perezi ... Hezroni ... Karmi ... Huri ... Shobali ... Reaia ... Yahathi ... Ahumai ... Lahadi

Haya ni majina ya wanaume

Zora

Hili kundi la watu liliitwa kwa jina la mji wa Zora walipoisi

1 Chronicles 4:3

Hawa walikuwa mababu

Hii ya husu orodha ya mistari ya awali. Ingawa, baadhi ya tafsiri ya husisha haya majina katika mahusiano ya baba-mwana. Katika namna hii, baadhi ya tafsiri ya husisha Penueli kama baba wa Gedori, badala ya muanzilishi wa ukoo wa Gedori.

Etamu ... Gedori ... Husha

Hay ni majina ya miji.

Ishma ... Idbashi ... Penueli ... Ezeri ... Efrathi

Haya ni majina ya wanaume.

Haselelponi

Hili ni jina la mwanamke.

Hawa walikuwa uzao wa Huri

"Penueli na Ezeri walikuwa uzao wa Huri." Hii ya tanguliza orodha itayofuata.

1 Chronicles 4:5

Ashuri ... Tekoa ... Ahuzamu ... Heferi ... Serethi ... Ishari ... Ethnani ... Kozi ... Anubu ... Zobeba ... Aharheli ... Harumu

Haya ni majina ya wanaume.

Temeni ... Ahashatari

Haya hapa yana fahamika kama majina ya wanaume. Ingawa, baadhi ya tafsiri inayaelewa kama majina ya koo zilizo anzishwa na Ashuri.

Hela ... Naara

Haya ni majina ya wanawake.

alimzalia

"aliwaza wana wake"

a koo zilizotoka kwa Aharheli mwana wa Harumu

Sentensi mpya ya anza hapa. "Kozi pia akawa babu wa Harumu na koo zilizotoka kwa Harumu mwana wa Aharheli"

1 Chronicles 4:9

Yabesi

Hili ni jina la mwanaume.

ongeza mipaka yangu

"nipe mimi eneo zaid"

mkono wako ukuwa juu yangu

Baadhi ya maana ni kwamba mkono wa Mungu wa wakilisha 1) muongozo wake, 2) nguvu zake, au 3) ulinzi wake. "nilinde mimi" au "nifanye ni fanikiwe" au "nilinde." Pia yaweza tafsiriwa kwa ujumla kama "kuwa na mimi."

akamjalia maombi yake

"akafanya sawa na maombi yake"

1 Chronicles 4:11

Kelubu ... Shuha ... Mehiri ... Eshtoni ... Bethi - Rafa ... Pasea ... Tehina

Haya ni majina ya wanaume.

Tehina, ambaye alianzisha mji wa Nahashi

"Tehina, mwanzilishi wa mji wa Nahashi"

Nahashi

Hili ni jina la mji.

Reka

Hili ni jina la sehemu.

1 Chronicles 4:13

Maelezo ya jumla

Itasaidia kutengeneza muunganiko wa mstari na kuweka mstari wa 15 pamoja na mstari wa 13 maana Kenazi alikuwa mzao wa Yefune na Kalebu.

Kenazi ... Othinieli ... Seraia ... Hathathi ... Meonothai ... Ofara ... Yoabu ... Yefune ... Iru ... Ele ... Namu ... Yehaleli ... Zifi .. Zifa ... Tiriya ... Asareli

Haya ni majina ya wanaume.

Ge Harashimu, ambaye watu wake walikuwa wahunzi

Ge Harashimu ina maana ya "Bonde la Wahunzi". Maana ya jina ya weza tafsiriwa au ya weza kufanywa kama lilivyo na maelezo yake: "Ge Harashimu, lenye maana ya 'Bonde la Wahunzi.' Liliitwa hivi sababu watu wake walikuwa wahunzi."

Wahunzi

watu walio na ujuzi wa kutengeneza au kujenga vitu

1 Chronicles 4:17

Maelezo ya Jumla

Maelezo ya 4:17 yamepangiliwa tena ili maana yake ieleweke kwa urahisi zaidi.

Ezra ... Yetheri ... Meredi ... Eferi ... Yaloni ... Miriamu ... Shamai ... Ishibahi ... Eshitemoa ... Yeredi ... Gedori ... Heberi ... Soko ... Yekuthieli ... Zanoa

Haya ni majina ya wanaume.

Hawa walikua wana wa Bithia

Neno "hawa" la mtaja Miriamu, Shamai, na Ishibahi. Walikuwa wana Bithia aliye mzalia mme wake Meredi.

Bithia

Hili ni jina la mwanamke.

Mke wa Kiyahudi wa Meredi

Maandishi ya Kiebrania yasema, "Mke wake wa Kiyahudi," lakini tafsiri nyingi za elewa "wa" ya mhusu Meredi. Hii ya taja mke tofauti wa Meredi, ukiongeza kwa Bithia

1 Chronicles 4:19

Hodaia ... Nahamu ... Keila ... Eshtemoa ... Shimoni ... Amnoni ... Rina ... Ben Hanani ... Tiloni ... Ishi ... Zohethi ... Beni Zoheti

Haya ni majina ya wanaume.

Mgarimi

mtu wa kundi la wa Gari

Mmakathi

mtu kutoka eneo la Maka, linalo itwa pia Makathi.

1 Chronicles 4:21

Shela ... Er ... Leka ... Laada Maresha ... Yoakimu ... Yoashi ... Sarafi

Haya ni majina ya watu

wafinyanzi

watu wanao tengeneza mikebe kutokana na udogo

Bethi Ashbea ... Kozeba ... Netaimu ... Gedera

Haya ni majina ya wanaume

1 Chronicles 4:24

Nemueli ... Yamini ... Yaribu .. Zera ... Shauli ... Shalumu ... Mibsamu ... Mishima ... Hamueli ... Zakuri ... Shimei

Haya ni majina ya wanume

mjukuu

mwana wa mtoto wa mtu

kitukuu

mjukuu - mwana wa mjukuu wa mtu au mjukuu wa kike

1 Chronicles 4:27

wana kumi na sita na mabinti sita

"wana 16 na mabinti 6"

Molada ... Hazari Shuali

Haya ni majina ya miji.

1 Chronicles 4:29

Maelezo ya Jumla

Orodha ya miji ya uzao wa Simeoni uliishi ya endelea

Bilha, Ezemu, Toladi, Bethueli, Horma, Zikilagi, Bethi Markabothi, Hazari Susimi, Bethi Biri, Shaaraimu

Haya ni majina ya miji.

1 Chronicles 4:32

Maelezo ya Jumla

Orodha ya sehemu uzao wa Simeoni uliishi yaendelea.

Etamu ... Aini .. Rimoni ... Tocheni ... Ashani

Haya ni majina ya vijiji.

mipaka

mbali na idadi kubwa ya watu

1 Chronicles 4:34

Meshobabu, Yamileki, Yoshahi mwana wa Amazia, Yoeli, Yehu mwana wa Yoshibia mwana wa Seraia, Asieli, Elioenai, Yaakoba, Yeshohaia, Asaia, Adieli, Yesimieli, Benaia, Ziza, Shifi, Aloni Yedaia Shimiri Shemaia

Haya ni majina ya wanaume

Hawa walio orodheshwa kwa majina walikua viongozi

"Hawa wanaume walikuwa viongozi"

koo zao ziliongezeka sana

idadi ya watu kwenye koo zao iliongezeka sana"

1 Chronicles 4:39

Gedori

Hili ni jina la mji

malishoni

eneo ambao wanyama wana kula nyasi

mengi

kiasi kikubwa

Wahami

uzao wa Hamu

Wameuni

Hili ni jina la kundi la watu. "uzao wa Meuni"

1 Chronicles 4:42

Wanaume mia tano

"wanaume 500"

Pelatia, Nearia, Refaia, Uzieli, Ishi

Haya ni majina ya watu.

wakimbizi wa Waamaleki waliobakia

"wakimbizi walio baki"

wakimbizi

watu walio lazimishwa kuondoka nchini kwao

hadi siku hii

"kutoka kwao hadi sasa"

1 Chronicles 5

1 Chronicles 5:1

sasa Ruben

Neno "sasa" limetumika hapa kuweka alama ya mabadiliko kutoka orodha ya uzao hadi maelezo ya awali ya Rubeni

lakini haki yake ya mzaliwa wa kwanza ilipewa kwa wana wa Yusufu mwana wa Israeli

"lakini Israeli aliwapa haki ya mzaliwa wa kwanza ya Rubeni kwa wana wa Yusufu, mwengine wa watoto wa Israeli"

Rubeni alinajisi kochi la baba yake

Hii ni namna ya adabu ya kusema kuwa Rubeni alilala na mke wa pili wa baba yake. Kochi ni sehemu mwanaume na mke wake walilala pamoja.

Hivyo hajanakiliwa kama mwana wa kwanza

"Hivyo historia ya familia ya haimuorodheshi Rubeni kama mwana mkubwa"

Hanoki, Palu, Hezroni, Karmi

Haya ni majina ya wanaume

1 Chronicles 5:4

Yoeli ... Shemaia ... Gogi ... Shimei ... Mika Reaia ... Reaia ... Baali ... Bera ... Tiligathi Pileser

Haya ni majina ya wanaume

Tiligath Pileseri

Hili jina limeandikwa pia kama Tiglathi Pileaseri katika sehemu zingine za Biblia

1 Chronicles 5:7

wameorodheshwa katika nakala za uzao wao

Hii yaeza anza sentensi mpya: "Nakala zao za uzao zimewaorodhesha kama"

nakala za uzao

nakala zinazoonyesha jinsi watu katika familia wanavyo husiana wao kwa wao

Yeieli ... Zekaria ... Bela ... Azazi ... Shema

Haya ni majina ya wanaume

Aroeri ... Nebo ... Baali Meoni

Haya ni majina ya miji

1 Chronicles 5:10

Wahagiri

Haya ni majina makundi ya watu.

1 Chronicles 5:11

Saleka

Hili ni jina la mji

Yoeli ... Shafamu ... Yanai ... Shafati ... Mikaeli ... Meshulamu ... Sheba ... Yorai ... Yakani ... Zia ... Eberi

Haya ni majina ya wanaume

1 Chronicles 5:14

Abihaili ... Huri ... Yaroa ... Gileadi ... Mikaeli ... Yeshishai ... Yado ... Buzi ... Ahi ... Abdieli ... Guni

Haya ni majina ya wanaume

1 Chronicles 5:16

Waliishi

"Kabila la shule liliishi"

nchi za malisho

maeno wanyama wanayo kula nyasi

Hawa wote waliorodheshwa katika nakaka za uzao

"Nakala za uzao ziliwaorodhesha wote" au "Nakala zao familia za mababu ziliwaorodhesha"

Hawa wote

Haiko wazi ni idadi gani ya watu walio tangulia imetajwa

1 Chronicles 5:18

Warubeni

Hii ya husu watu kutoka kabila la Rubeni

Wagadi

Hii ya husu watu kutoka kabila la Gadi

wana jeshi elfu arobaini na nne

wana jeshi elfu nne "44, 000 soldiers"

walio beba ngao na upanga, na pinde na mishale

Wanajeshi wanaelezwa kama wenye ujuzi vitani kwa silaha walizo beba. "Walifunzwa kupambana vizuri vitani"

Wahagri ... Yeturi ... Nafishi ... Nodabu

Haya ni majina ya makundi ya watu.

1 Chronicles 5:20

Waisraeli walipaza sauti kwa Mungu

"Waisraeli walimuomba Mungu kwa sauti kwa ajili ya Msaada"

Walikamata

"Waisraeli walikamata Wahagri"

ngamia elfu hamsini

"ngamia 50,000"

punda elfu mbili

"punda 2,000"

Kwa sababu Mungu aliwapigania

Msaada wa Mungu waelezwa kama mwanajeshi aliye pigana vitani. "Kwasababu Mungu aliwasaidia"

1 Chronicles 5:23

Baali Herimoni ... Seniri

Haya ni majina ya milima

Eferi, Ishi, Elieli, Azrieli, Yeremia, Hodavia, na Yahdieli

Haya ni majina ya wanaume

1 Chronicles 5:25

Puli ... Tiligathi Pileseri

Haya ni majina ya wanaume

Warubeni ... Wagadi

Haya ni majina ya makundi ya watu

Hala ... Habori ... Hara

Haya ni majina ya miji

Gozani

Hili ni jina la mto

1 Chronicles 6

1 Chronicles 6:1

Gerishoni ... Kohathi ... Merari ... Amramu ... Izhari ... Hebroni ... Uzieli ... Nadabu ... Abihu ... Eleazari ... Ithamari

Haya ni majina ya wanaume.

1 Chronicles 6:4

Eleazari ... Abishua ... Buki ... Uzi ... Zerahia ... Meraioti

Haya ni majina ya wanaume.

1 Chronicles 6:7

Meraioti ... Amaria ... Ahitubi ... Zadoki ... Ahimazi ... Yohanani

haya ni majina ya wanaume.

1 Chronicles 6:10

Amaria ... Ahitubi ... Zadoki ... Shalumu

Haya ni majina ya wanaume.

1 Chronicles 6:13

Hilikia ... Seraia ... Yehozadaki

Haya ni majina ya wanaume.

wapeleka utumwani Yuda na Yerusalemu kwa mkono wa Nebukadneza.

Nguvu ya Nebukadneza kupitia jeshi lake inafafanuliwa kama sehemu ya mwili wake ("mkono") alitumika kuongoza jeshi lake. " aliruhusu jeshi la Nebukadneza kushinda majeshi ya Yuda na Yerusalemu na kuchukua watu kwenda matekani."

1 Chronicles 6:16

Gershomi ... Kohathi ... Merari

Ona jinsi ulivyo tafsiri haya majina 6:1

Libni ... Shimei

Haya ni majina ya wanaume

Amramu ... Izhari ... Hebroni ... Uzieli

Ona jinsi ulivyo tafsiri haya majina 6:1

1 Chronicles 6:19

Merari ... Mahili ... Mushi ... Yahathi ... Zima ... Yoa ... Ido ... Zera ... Yeatherai ...

Haya ni majina ya wanaume

1 Chronicles 6:22

Aminadabu ... Kora ... Asiri ... Elikana ... Ebiasa ... Tahathi ... Urieli ... Uzia ... Shauli

Haya ni majina ya wanaume

1 Chronicles 6:25

Elikana ... Amasai ... Ahimothi ... Zofai ... Nahathi ... Eliabu .. Yerohamu

Haya ni majina ya wanawake

1 Chronicles 6:28

Yoeli ... Merari ... Mahli ... Libni ... Shimei ... uza ... Shimea ... Hagia ... Asaia

Haya ni majina ya wanaume

mzaliwa wa pili

"wana wa pili kuzaliwa"

1 Chronicles 6:31

sanduku kuja hapo

"watu wa Israeli walieka sanduku kule"

hema, hema la kukutania

Maana kadha ni 1) kwamba "hema la kukutania" la eleza jina lingine la "maskani" (UDB) au 2) "eneo takatifu la hema la kukutani"

Walikamilisha wajibu wao kwa kadiri ya maelekezo waliopewa

"Waimbaji walitii maelekezo ya Daudi"

1 Chronicles 6:33

Hawa

"Hawa walikuwa wana muziki"

Wakohathi

Hili ni jina la kundi la watu

kurudi nyuma ya wakati

Hii ina maana orodha inaenda kutokana na wa hivi karibuni na wa zamani.

Hemani ... Yerohamu ... Elieli ... Toa ... Zufi ... Mahathi

Haya ni majina ya wanaume.

Elikana ... Amasai

Ona jinsi ulivyo tafsiri haya majina ya hawa wanaume 6:25

1 Chronicles 6:36

Tahathi ... Asiri ... Ebiasa .. Izhari ... kohathi

Haya ni majina ya watu

1 Chronicles 6:39

Berekia ... Shimea ... Mikaeli ... Baaseia ... Malikiya ... Ethani ... Zima ... Shimei Yahathi ... Gerishomu

Haya ni majina ya watu

Msaidizi

"mfanya kazi mwenza"

aliye simama mkono wake wa kuume

Mamlaka ya mtu yaelezwa kama kwa wapi wanapo simama. Mkono wa kulia wa mtu ni sehemu mtu mwenye mamlaka alisimama.

1 Chronicles 6:44

mkono wa koshoto wa Heman

"Kusimama mkono wa kushuto wa Hemani"

Msaidizi

"Mfanya kazi mwenza"

1 Chronicles 6:48

Walawi, alipangiwa kufanya

"Ilikuwa ni kazi ya wafanya kazi wenza, Walawi, kufanya"

1 Chronicles 6:49

izi sadaka zilifanya maombezi kwa ajili ya Waisraeli

"Hizi sadaka zilikuwa za kufanya maombezi kwa dhambi za watu wa Israeli"

1 Chronicles 6:50

Uzao wa Aruni una kumbukwa kama ifuatavyo

"Hawa walikuwa uzao wa Aruni"

1 Chronicles 6:54

Hizi ni sehemu ambazo wazao wa Aruni walipangiwa kuishi, wazao wa Aruni ambao walitoka katika koo za Wakohathi (maeneo ya kwanza yalikuwa yao)

"Haya ndiyo maeno ambayo uzao wa Aruni, koo za Wakohathi, waliishi (kura zilpigwa kujua wapi wataishi)"

Wakohathi

Ona jinsi ulivyo tafsiri 6:33

Walipewa Hebron

"Waliwapatia Hebroni kuwa yao"

lakini maeneo ya mji na vijiji alipewa Kalebu mwana wa Yefune

"Kalebu na familia yake walienda kuishi kwenye mashamba ya Hebroni na vijiji vizungukavyo"

nchi ya malisho

Hii ni sehemu ya nyasi ambapo wanyama wanakula.

1 Chronicles 6:59

Jumla ya miji yao ilikuwa kumi na tatu

"Walikuwa na jumla ya miji kumi na tatu"

1 Chronicles 6:61

Gerishomu kwa koo zao tofauti walipewa miji kumi na tatu

"Koo za Gerishomu uzao wake ulipata miji 13"

Kohathi ... Gerishomu

Ona jinsi ulivyo tafsiri 6:1

1 Chronicles 6:63

Merari

Ona jinsi ulivyo tafsiri 6:1

miji iliyo tajwa awali kutoka

"hiyo miji kutoka"

1 Chronicles 6:66

Wakohathi

Ona jinsi ulivyo tafsiri 6:33

1 Chronicles 6:71

Gerishomu

Ona jinsi ulivyo tafsiri 6:1

1 Chronicles 6:77

Merari

Ona jinsi ulivyo tafsiri 6:1

Merari ... nchi ya malisho

"kabila la Zebuluni ili wapa uzao wa Merari Rimono na nchi yake yamalisho na Tabori na nchi yake ya Malisho"

Kwa wao pia walipewa ... kabila la Rubeni

Maelezo katika 6:77 yamepangiliwa tena ili maana yake iweze kueleweka kwa uraisi.

Kwa wao pia walipewa

"Pia walipata zaidi"

1 Chronicles 7

1 Chronicles 7:1

walikua na idadi ya 22,600

"Walikuwa wanaume elfu ishirini na mbili na mia sita"

Katika siku za Daudi

"kipindi cha maisha ya Daudi

1 Chronicles 7:4

Pamoja nao walikua na

"Miongoni mwao walikuwa"

jeshi la watu elfu thelathini na sita kwa mapambano

wana jeshi elfu sita kwa pambano - "wana jeshi 36,000 walio kuwa tayari kwa pambano"

1 Chronicles 7:6

waanzilishi

"baba" au "mababu"

1 Chronicles 7:11

Yedieli ... Iri ... Aheri

Haya ni majina ya wanawake

Waliorodheshwa katika ukoo orodha ilikuwa 17,200

"Orodha ya ukoo ilikuwa na elfu kumi na saba na mia mbili"

Shupimu ... Hupimu ... Hushimu

Haya ni majina ya wanaume

1 Chronicles 7:13

Yazieli, Guni, Yezeri, na Shalumu

Haya ni majina ya wanaume

wajukuu wa Bilhahi

"wana wa wana wa Bilhahi"

1 Chronicles 7:14

Waarami

Hii yaeleza mtu wakutoka Aramu, eneo la Syria

suria wake wa Kiaramia alimzalia

"Suria wa Kiaramia alimza"

1 Chronicles 7:20

Eza na Eleadi waliuawa na wanaume wa Gati, wenyeji wa nchi

"Wanaume wa Gathi, wenyeji wa nchi, waliwaua Eza na Eleadi"

walipoenda kuiba mifugo yao

"ndugu walienda kuiba mifugo kutoka kwa watu wa Gathi"

1 Chronicles 7:23

Akapata mimba akamzaa mwana

"Alishika mimba na kuzaa mwana"

akamuita

"alimpa jina"

Beria ... Sheera

Haya ni majina ya watu

juu na chini Beth Horon na Uzzen Sheerah

Haya ni majina ya sehemu.

1 Chronicles 7:28

makazi yao yalikuwa

"nyumbani kwao kulikuwa"

atika huu mji waliishi uzao wa Josefu mwana wa Israeli

"Uzao wa Yusufu, mwana wa Israeli, waliishi kwenye hii miji"

1 Chronicles 7:39

wananume wa kipekee

"wanaume muhimu"

Kulikuwa na wanaume elfu ishirini na sita walioorodheshwa waliokuwa imara kwa kazi ya jeshi, kwa mujibu wa idadi iliyo orodheshwa

wanaume elfu sita waliorodhesha walikuwa tayari kwa ajili ya kazi ya jeshi, kwa mujibu wa idadi ya orodha* "Kwa mujibu wa nakala za koo, walikuwa 26,000 wanaume wanao weza kutumika kwenye jeshi.

1 Chronicles 8

1 Chronicles 8:6

walihimizwa kuhamia

"waliitaji kuhama" au "waliitaji kuhama"

1 Chronicles 8:8

Shaharaimu ... Yobabu ... Zibia ... Mesha ... Malkamu ... Yeuzi ... Shachia ... Mirima ... Abitubi ... Elipaali

Haya ni majina ya wanaume

Hushimu ... Baara ... Hodeshi

Haya ni majina ya wanawake

kwa mke wake Hodeshi, Shaharaimu akawa baba wa

"Shaharaimu na mkewe Hodeshi walikuwa na wana wafuatao"

1 Chronicles 8:12

Elipaali ... Eberi ... Mishamu ... Shemedi ... Beria ... Shema

Haya ni majina ya wanaume.

Ono ... Lodi ... Aijaloni

Haya ni majina ya sehemu

1 Chronicles 8:14

Elipaali ... na Yobabu

Maelezo katika 8:14 yamepangiliwa tena ili maana yake ieleweke kwa urahisi zaidi.

1 Chronicles 8:19

Maelezo ya Jumla

Maelezo katika 8:19 yamepangiliwa tena ili maana yake ieleweke kwa urahisi zaidi.

1 Chronicles 8:22

Maelezo ya Jumla

Maelezo katika 8:22 yamepangiliwa tena ili maana yake ieleweke kwa urahisi zaidi.

1 Chronicles 8:26

Hawa walikuwa vichwa vya koo na viongozi

Maneno "vichwa vya familia" na "viongozi" ina maana moja.

1 Chronicles 8:29

Baba wa Gibeoni, Jeieli, ambaye mke wake aliitwa Maaka, aliishi ndani ya Gibeoni

Hapa "baba wa" ya husu hali ya Wayahudi kama kiongozi wa mji wa Gibeoni. "Yeieli, kiongozi wa Gibeoni, aliishi Gibeoni. Jina la mkewe lilikuwa Maaka"

Uzao wake wa kwanza

"mzaliwa wa kwanza wa Yeieli"

1 Chronicles 8:38

Yeushi wa pili, na Elifeleti wa tat

"Yeushi mwana wa 2, na Elifeleti wa tatu"

Walikuwa na wana wengi na wajukuu, jumla ya 150

"Walikuwa na jumla ya wana mia na hamsini na tano na wajuu"

1 Chronicles 9

1 Chronicles 9:1

Kwa hivyo watu wote wa Israeli walinakiliwa ki uzao

Nakala ya uzao yaeleza kumbukumbu ya uzao wa familia au mababu wa mtu.

Walinakiliwa katika vitabu vya kifalme vya Israeli

Hii ya husu kitabu ambacho hakipo tena.

1 Chronicles 9:4

Washiloni

Hili ni jina la group lilitoka Shela.

1 Chronicles 9:12

Walikuwa ni wanaume wenye uwezo sana wa kufanya kazi katika nyumba ya Mungu

Hawa wanaume wenye uwezo walifanya kazi katika nyumba ya Mungu"

1 Chronicles 9:14

Shemaia ... Elikana

Haya ni majina ya wanaume

kati ya uzao

"mmoja wa uzao"

Wanetofa

Hili ni jina la kundi la watu.

1 Chronicles 9:17

Walinzi wa lango

"askari" au "walinzi wa lango"

Awali walisimama kulinda katika geti la mfalme upande wa mashariki wa kambi ya uzao wa Walawi

"Uzao wa Walawi ulilinda lango la mfalme upande wa mashariki ya kambi"

mlango wa hema ... ango la kuingilia

Haya maneno yote yanaelezea mwingilio wa hema ya kukutania, au maskani

1 Chronicles 9:20

aliwaongoza

"aliwaongoza maaskari"

1 Chronicles 9:22

Majina yao yaliandikwa kwenye kumbukumbu za watu katika vijiji vyao

"Nakala zao katika vijiji vya hawa watu vilijumuisha majina ya hawa wanaume

watoto wao

"uzao wao"

Walinzi wa mageti waliwekwa

"wanaume walilinda miingilio"

pande zote nne, upande wa mashariki, magharibi, kaskazini, na kusini

"pande zote"

1 Chronicles 9:25

Kaka zao

"kaka za walinzi"

walikuja kuwasaidia baada ya mzunguko wa siku saba

mzunguko wa siku, wa awamu "walikuja kusaidia kwa mzunguko wa siku 7, wakipeana awamu"

walipangiwa kulinda vyumba

"walilinda vyumba"

1 Chronicles 9:28

Baadhi yao

"Baadhi ya askari"

walihesabu makala zilizo ingizwa ndani na zilizo tolewa nje

"walihesabau makala watu waliotoa nje kutumia, na wakahesabu makala watu walipo rudisha"

waliwekwa kutunza

"kutunza" au "kujali"

1 Chronicles 9:30

Matithia ... Shalumu

Haya ni majina ya watu.

Wakorahi ... Wakohathi

Haya ni majina ya makundi ya watu.

mikate ya uwepo

Ona kurasa ya neno kuhusu "mkate" kwa maelezo fasii kuhusu "mkate wa uwepo"

1 Chronicles 9:33

walipo kuwa hawafanyi kazi

"hawakuwa na haja ya kufanya kazi nyingine"

kufanya kazi walio pangiwa

"waliitaji kukamilisha kazi yao ya kupangiwa"

usiku na mchana

Hii ina maanisha "wakati wote" na ya weza kufasiriwa kwa kutumia maneno au neno kutoka lugha yako au tamaduni yako yenye kuleta maana moja

Hawa walikuwa viongozi wa familia miongoni mwa Walawi, kama ilivyo orodheshwa katika kumbukumbu za uzao wao

" Historia ya familia orodha yake yataja majina ya Walawi viongozi wa familia"

1 Chronicles 9:35

Gibeoni

Maelezo ya kwanza ya Gibeoni ya eleza mtu lakini ya pili ya taja mji.

1 Chronicles 10

1 Chronicles 10:1

Kila mwanaume wa Israeli alikimbia Wafilisti

"Jeshi la Waisraeli liliwakimbia kutoka"

kuanguka na kufa

"kufa"

1 Chronicles 10:4

unichome nao

"niue nao"

Lasihivyo, hawa wasio tahiriwa watukuja

Maelezo kuhusu "wasio tahiriwa" hapa ni kashfa, ikihashiria kuwa hawa watu ni wageni na hawana mahusiano na Mungu.

kuangukia

"alijiua nao"

1 Chronicles 10:5

a wana wake watatu

"na wana wake wa 3 wakafa"

1 Chronicles 10:7

Kila mwanaume wa Israeli

"Wanaume wa Israeli walipo"

kuishi humo

"waliishi katika miji ya Waisraeli"

Ikawa siku

Hili neno hapa la tumika kueka alama ya tukio muhimu katika historia. Kama lugha yako ina namna ya kufanya hivi, fikiria kutumia hapa.

kukagua wafu

"kuchukuwa kila kitu cha thamani miilini mwa wafu"

Sauli na wana wake wameanguka

"Sauli na wana wake wamekufa"

1 Chronicles 10:9

Wakamvu

"Wafilisti waliondoa kutoka mwilini mwa Sauli"

Ngao yake wakaeka

"Wafilisti wakachukuwa ngao ya Sauli"

Dagoni

Hili ni jina la mungu wa uongo.

1 Chronicles 10:11

Yabeshi Gileadi yote ilipo sikia Wafilisti waliyo

"Watu wa Yabeshi Gileadi walipo sikia nini wana jeshi wa Wafilisti"

mifupa yao

"miili yao" au "mabaki yao"

1 Chronicles 10:13

ushauri

Hii ni maoni au pendekezo kuhusu nini mtu afanye.

ngea na wafu

"alidai kuongea na hao walio kufa"

mwongozo

Hii ni msaada au ushauri kuhusu nini tufanye.

akamua na kupindua ufalme

"kuwapa uongozi wa watu wa Israeli kwa"

1 Chronicles 11

1 Chronicles 11:1

sisi ni nyama na mifupa yako

"sisi ni ndugu zako" au "tuna mababu sawa na wewe"

neno la Yahweh

"ujumbe wa Yahweh"

1 Chronicles 11:4

Yebusi

Hili lilikuwa jina fupi la Yerusalemu baada ya Wayebusi kuuteka mji, kabla ya Waisraeli kuchukuwa.

Daudi alichukuwa

"Lakini jeshi la Daudi lilishinda"

mji wa Daudi

"na wakauita mji wa Daudi"

hivyo akafanywa mkuu wa jeshi

"Hivyo Daudi akamfanya Yoabu mkuu"

1 Chronicles 11:7

Akaimarisha mji

"Waisraeli wakafanya ukuta kuuzunguka mji imara"

kutoka Milo

Hii yaeleza ngome ya Yerusalemu, labda iliyo tengenezwa na Wayebusi.

alikuwa naye

"alimsaidia"

1 Chronicles 11:10

viongozi Daudi aliyo kuwa nao

"viongozi chini ya Daudi"

waliyo jionyesha imara katika ufalme wake

"aliyo saidia uongozi wa Daudi kubaki imara"

thelathini

"wanaume hodari 30"

katika sehemu moja

"kwa wakati mmoja"

1 Chronicles 11:12

na kuwakata Wafilisti

"na kuwaua wafilisti wengi"

1 Chronicles 11:15

watatu wa viongozi thelathini

"3 wa 30"

Kwa wakati huo Daudi alikuwa katika ngome yake, pangoni, Wafilisti walikita kambi yao Bethilehemu

Daudi alikuwa sehemu salama katika pango wakati wana jeshi Wafilisti wakilinda Bethlehemu"

Wafilisti walikita kambi yao Bethilehemu

"Wafilisti waliweka wana jeshi Bethilehemu"

1 Chronicles 11:18

wanaume hodari watatu

wanaume hodari 3"

kisima cha Bethilehemu, kisima pembeni mwa lango

Haya maneno mawili yanahusu kisima kimoja. Ya pili ya husu kisima gani Bethilehemu.

Yahweh, iwe mbali na mimi, kwamba ni yanywe haya maji

Mungu, tafadhali usiniache ninywe dhabihu kama hii kwa gharama ya wanaume wangu"

Je ninywe damu ya wanaume walio hatarisha maisha yao?

Daudi anasema kwa swali kuwa maji yana dhamani kwasababu ya dhabihu iliyo tolewa na hao walioenda kufuata. "Sitakunywa damu ya wanaume walio radhi kufa kwa ajili yangu" au "Sitakunywa maji wanaume walio hatarisha maisha yao kuyapata"

1 Chronicles 11:20

wa watatu

"mashujaa Watatu"

alikuwa kiongozi wa watatu

"Abishai alikuwa kiongozi wa mashujaa watatu

yeye alipewa heshima mara mbili na akawa kiongozi wao

"wana jeshi walikuwa na heshima kubwa kwa Abishai na wakamfanya kiongozi, japo hawaku mhesabu kama kiongozi wa mashujaa Watatu"

1 Chronicles 11:22

mambo makuu

Haya ni matendo yanayoonyesha ujasiri, uweza, au ujuzi.

theluji ikianguka

"wakati wa dhoruba ya theluji"

lakini alimfuata chini

"Benaia alikutana na Mmisri"

mkuki kama gongo la mshonaji

"mkuki mkubwa sana"

1 Chronicles 11:24

akatajwa miongoni mwa wale wanaume hodari watatu

"alikuwa maarufu kama wanaume hodari 3"

Alisifika zaidi ya wale wanajeshi thelathini kwa ujumla, lakini hakuwa pewa hadhi ya wale wanajeshi watatu hodari

"Watu walimheshimu kuliko wana jeshi wale 30, lakini sio zaidi ya wale 3 wenye ujuzi wa juu"

walinzi

Huyu ni mtu au kundi la watu wenye wajibu wakumlinda mtu muhimu.

1 Chronicles 11:42

thelathini pamoja nae

"wanaume 30 pamoja nae"

1 Chronicles 12

1 Chronicles 12:1

wakati akiwa bado amefukuzwa katika uwepo wa

"wakati alipo kuwa hawezi kuwa katika uwepo wa"

Walikuwa wana upinde na waliweza kutumia mkono wa kuume na wakushoto

"Silaha zao zilikuwa upinde, na waliweza kutumia upinde kwa mkono wa kulia au wakushoto"

mawe na manati

Manati ilizungushiwa ngozi iliyo mruhusu mtu kutupa jiwe kwa umbali mrefu. Jiwe liliwekwa katikati wakati mtu alishika miisho na kuzungusha kwa duara. Alipo achilia, jiwe liliruka palipo lengwa.

1 Chronicles 12:3

wale thelathini

"wale wana jeshi 30"

1 Chronicles 12:8

ambao nyuso zao zilikuwa kali kama za simba

"walio kuwa wakali sana"

Walikuwa wepesi kama swala

"Walikuwa wana mbio sana"

swala

Hawa ni wanyama walio wa pole na wepesi, mfano wa ayala.

1 Chronicles 12:9

wapili ... wakumi na moja

Hii ya waorodhesha hawa wanaume kwa vyeo vya uongozi. "2 ... 3 ... 4 ... 5 ... 6 ... 7... 8 ... 9 ... 10 ... 11"

1 Chronicles 12:14

Wamwisho aliongoza mia moja

Hii ina maana kuwa kundi dogo kiongozi alilo ongozi ni 100.

mkubwa aliongoza elfu moja

Hii ina maana kuwa kundi kubwa kiongozi alilo ongozi ni 1000.

mwezi wa kwanza

Huu ni mwezi wa kalenda ya Kiebrania. Ni wakati wa mwisho wa Machi na sehemu ya kwanza Aprili kwa kalenda za magharibi. Ni mwanzo wa masika mvua za mwisho zaja.

1 Chronicles 12:16

wanaume wa Benjamini na Yuda

"wanaume kutoka kabila la Benjamini na Yuda"

1 Chronicles 12:18

roho ikaja juu ya

"Roho ikampa nguvu"

wale thelathini

"wale 30"

Sisi ni wako, Daudi. Sisi tupo upande wako, mwana wa Yesse

Haya maneno ya shiriki maana moja na mkazo wa kumfuata Daudi.

1 Chronicles 12:19

Atamwendea

"kuwaacha viongozi wao kujiunga na"

wa maelfu

"Zaidi ya wanaume 1000"

1 Chronicles 12:21

kikundi cha wezi

"makundi ya watu waliyo wapora nchi nzima"

kama jeshi la Mungu

Hii inalinganisha ukubwa wa jeshi la Daudi kwa jeshi la malaika wa Mungu.

1 Chronicles 12:23

uupindua ufalme wa Sauli kwake

"kumpa utawala wa Sauli kwa Daudi"

ilikutimiza neno la Yahweh

"walifanya neno la Yahweh kweli" au "kutimiza neno la Yahweh"

Kutoka Yuda

"Kutoka kabila la Yuda"

1 Chronicles 12:29

Kutoka kwa Benjamini, kabila la Sauli

"Kutoka kabila la Yuda, kabila la Benjamini"

nusu kabila

Ona jinsi ulivyo tafsiri 5:18

1 Chronicles 12:36

wameandaliwa na silaha za kila namna

"wabeba silaha za kila namna"

1 Chronicles 12:38

dhumuni maalumu

"mipango"

waliandaliwa kwa pambano

"kwa silaha zao kwa ajili ya vita"

siku tatu

"siku 3"

zabibu kavu

Haya ni mizabibu iliyo kaushwa, tunda dogo linalo kuwa kwenye mzabibu

1 Chronicles 13

1 Chronicles 13:1

maelfu na mamia

Jeshi lilikuwa na wakuu walio waongoza makundi ya wana jeshi wa kila kimo. "zaidi ya wanaume 1000 na zaidi ya wanaume 100"

yalionekana sawa machoni pa watu wote

Hapa "macho yana wakilisha mawazo na maoni ya watu. "watu wote walidhani haya ni mambo sahihi ya kufanya"

1 Chronicles 13:5

Baala

Hili ni jina lingine la Kiriathi Yearimu.

ambaye ameketi juu ya makerubi

"anaye tawala kutoka amri za viumbe wenye mabawa katika sanduku la agano"

1 Chronicles 13:7

chombo kipya cha matairi

Hili ni gari la matairi linalo vutwa na mnyama ambaye hajawai kutumika.

tari

chombo cha muziki chenye kichwa cha ngoma kinacho weza kupigwa na chenye vipande vya chuma vilivyo zunguka vinavyo toa sauti ngoma inapo pigwa.

upatu

nyembamba, sahani za chuma zinazo gonganishwa pamoja kufanya sauti kubwa

1 Chronicles 13:9

Hasira ya Yahweh ikawaka juu ya Uza

"Yahweh alikuwa na hasira sana kwa Uza"

mbele za Mungu

"katika uwepo wa Mungu"

Daudi alipatwa na hasira

Daudi alishikwa na hasira dhidi ya Yahweh

hadi leo

Ona ulivyo tafsiri 4:42

1 Chronicles 13:12

Nawezaje kuleta sanduku la Mungu nyumbani mwangu?

Daudi anaeleza hasira yake kuhusu kifo cha Uza alipo kuwa ana jaribu kurudisha sanduku kwenye mji wake. "Siwezi kurudisha sanduku la Mungu kwenye mji wangu" au "Niambie Sheria za kurudisha sanduku, sijui jinsi ya kufanya hivi"

miezi mitatu

"miezi 3"

1 Chronicles 14

1 Chronicles 14:1

Hiramu

Jina la mfalme

maseremala

Hawa ni watu ambao kazi yao ni kufanya vitu vya mbao.

wajenzi

Hawa ni watu wa kufanya vitu kwa mawe au tofali.

alimfanya kuwa

"kumfanya"

ufalme wake ulitukuzwa juu sana kwa ajili ya watu wa Israeli

"Yahweh alimpa Daudi heshima katika ufalme wake kuwasaidia watu wa Israeli"

1 Chronicles 14:8

Daudi amepakwa mafuta kama mfalme juu ya Waisrael

"watu wa Israeli walimpaka mafuta Daudi kuwa mfalme wao"

bonde la Refaimu

Hili ni jina la sehemu

1 Chronicles 14:10

nitawakabidhi kwako

"nitakupa ushindi juu yao"

Baali Perazimu

Hili ni jina la sehemu

kwa mkono wangu

Hii ya husu vifaa vya Daudi. "kutumia jeshi langu"

kama vile mpasuko wa mafuriko ya maji.

Nguvu na ushindi wa jeshi la Daudi wafananishwa na mpasuko wa mafuriko ya maji. "kwa urahisi"

wateketezwe kwa moto

"kuchoma miungu yao ya uongo"

1 Chronicles 14:13

bonde

"bonde la Refaimu"

Usiwashambulie kwa mbele

"kushambulia kwa mbele"

wazunguke kwa nyuma yao na uwajie kupitia misitu ya balisamu

"nenda kupita msitu wa balisamu na kuwashumbulia kwa nyuma"

balisamu

Huu ni aina ya mti

1 Chronicles 14:15

Maelezo ya Jumla

Mungu anaendelea kumjibu Daudi kwa swali lake.

atakutangulia kwenda

"ataenda mbele yako kukupigania"

Gezeri

Hili ni jina la mji

umaarufu wa Daudi ukaenda katika nchi zote

"Watu wa mbali wakaskia ushinde wa Daudi dhidi ya Wafilisti"

1 Chronicles 15

1 Chronicles 15:1

Daudi akajingea nyumba zake

"Watu wakamjengea nyumba Daudi"

Akaanda sehemu

"akaamuru sehemu maalumu iandaliwe"

akakusanya Israeli yote

"akaamuru watu wote wa Israeli waje pamoja"

kuleta sanduku

"kusherehekea wakati Walawi wakibeba sanduku"

1 Chronicles 15:4

ndugu

watu walio wa sehemu ya familia au kabila moja

1 Chronicles 15:11

niliyo iandaa.

"Nimewaamuru Walawi kuianda"

1 Chronicles 15:13

Mara ya kwanza hamkubeba

"Hamkubeba sanduku kabla"

hatuku mtafuta

"hatukumuliza kwa maelekezo"

akawa na hasira kwetu

"akatuadhibu sisi"

Walawi waka jiweka wakfu iliwaweze kuleta

"Walawi walijisafisha ili kuweza kubeba"

1 Chronicles 15:16

upatu

Ona ulivyo tafsiri 3:7

wakipaza sauti zao

"kuimba"

daraja la pili

"mamlaka ya chini" au "darja la 2"

mlinzi wa lango

watu waliyo linda lango

1 Chronicles 15:19

upatu

Ona ulivyo tafsiri 3:7

waliongoza njia

"waliwaongoza wana muziki wengine" ua "waliongoza msafara"

1 Chronicles 15:25

wa maelfu

"zaidi ya wanaume 1000"

Obedi Edomu

Hili ni jina la mwanaume.

1 Chronicles 15:27

Daudi alivishwa joho safi la maridadi, pamoja na Walawi walio beba sanduku, waimbaji, na Kenania, kiongozi wa nyimbo na waimbaji

"Daudi, Walawi, na waimbaji wote walivaa mavazi safi ya majoho"

Joho

Hii ni aina nyororo, ya kitamba kigumu.

Kenania

Hili ni jina la mwanaume

Hivyo Israeli yote wakaleta sanduku la agano la Yahweh

"Hivyo umati mkubwa wa Waisraeli walileta sanduku la agano la Yahweh kutoka nyumba ya Obedi Edomu hadi Yerusalemu"

upatu

Ona jinsi ulivyo tafsiri 13:7

1 Chronicles 15:29

sanduku la Yahweh lilivyokuja kwa mji wa Daudi

"watu walileta sanduku la agano la Yahweh kwenye mji wa Daudi"

Mikali

Hili ni jina la mke wa Daudi

akamdharau moyoni mwake

"alimdharau sana katika fikra zake"

1 Chronicles 16

1 Chronicles 16:1

Wakaleta ndani Sanduku

"Waisraeli wakaleta sanduku"

kipande cha mkate

kipande kimoja cha mkate wa kuoka, wenye hamira

zabibu kavu

Hizi ni zabibu zilizo kavu, tunda dogo linalo ota kwenye mizabibu.

1 Chronicles 16:4

upatu

Ona ulivyo tafsiri 13:7

1 Chronicles 16:7

Kisha katika hiyo siku

Hii ya husu siku sanduku la agano liliamishwa kutoka nyumba ya Obedi Edomu kwenda Yerusalemu.

nyimbo ya shukurani

"nyimbo ya kutoa shukrani"

liitieni jina lake

"omba kwa Yahweh"

1 Chronicles 16:10

katika jina lake takatifu

"vile Mungu alivyo"

mioyo ya wanao mtafuta Yahweh

"acha hao wanaotaka kumjua Yahweh zaidi"

Mtafute Yahweh na nguvu zake; tafuteni uwepo wake siku zote

Haya maneno yanashiriki maana moja na yanatumika kutia mkazo. "Mtafute Yahweh na nguvu zake; tafuta kuwa karibu naye daima"

1 Chronicles 16:12

Kumbukeni matendo

"Kumbuka mambo mazuri"

kinywa chake

"aliyo nena"

3enyi uzao wa Israeli mtumishi wake, enyi watu wa Yakobo, wateule wake

Haya maneno yanashiriki maana moja na yanatumika kutia mkazo.

Amri zake zipo duniani kote

"Amri zake ni za watu wote wa dunia"

1 Chronicles 16:15

Tunzeni agano lake akilini mwenu

"Kumbuka agano la Yahweh"

vizazi elfu moja

"vizazi 1,000"

Anakumbuka

"Yahweh anakumbuka"

kama sehemu

"kama sehemu yako"

1 Chronicles 16:19

Nilisema hili mlipo kuwa wachache kwa idadi, wachache sana

"Yahweh alisema hili Waisraeli walipo kuwa kundi dogo la watu"

wageni katika nchi

"wageni katika nchi"

Walienda taifa hadi taifa, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine

Haya maneno yanashiriki maana moja na kutilia mkazo umbali Waisraeli walivyo tanga.

kwa ajili yao

"kwa sababu yao"

1 Chronicles 16:23

dunia yote

Kila kitu kwenye dunia cha leta utukufu kwa Mungu.

siku hadi siku

"kila siku"

1 Chronicles 16:25

Uzuri wa ajabu na utukufu upo uweponi mwake

"Uzuri na ajabu vimemzunguka"

Uwezo na furaha upo kwake

"Yahweh anaonyesha nguvu na furaha yake"

1 Chronicles 16:28

Mpeni sifa Yahweh

"Mpe sifa Yahweh kwa"

upasao jina lake

"anastahili au anastahili kupokea"

1 Chronicles 16:30

Mtetemeke mbele zake

"Onyesha hofu ya heshima kwa wazo lake"

Mbingu nazo ziwe nafuraha, na dunia ifurahi

"Acha kila mtu afurahi"

1 Chronicles 16:32

Bahari na ingurume

"Bahari itafanya sauti kubwa sana"

na inayo ijaza

"viumbe wa bahari"

miti iliyopo misituni ipige kele

Hii ina zungumzia miti kama ni watu wanao weza kupiga kelele kwa furaha.

1 Chronicles 16:34

Chema, wema

Neno "wema" lina maana tofauti kulingana na muktadha. Lugha nyingi zitatumia maneno tofauti kutafsiri hizi maana tofauti.

uaminifu wa agano, utii wa agano, upendo mwema, upendo usio shindwa

Hili neno la tumika kuelezea kujitolea kwa Mungu kutimiza ahadi alizo ziweka kwa watu.

dumu, kudumu

Neno "dumu" la maanisha kubaki kwa kipindi kirefu au kuvumili kitu kigumu kwa subira.

milele

Kwenye Biblia, neno "milele" la eleza muda usio kwisha. Wakati mwengine la tumika kifumbo kumaanisha, "muda mrefu sana"

Mungu

Katika Biblia, neno "Mungu" la husu kiumbe wa milele aliye umba ulimwengu bila chochote. Mungu yupo kama Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu. Jina la Mungu la binafsi ni "Yahweh"

wokovu

Neno "wokovu" la husu kuokolewa au kukombolewa kutoka kwenye uovu na hatari.

jina

Katika Biblia, neno "jina" linatumika kwa mfumbo kadhaa.

Kuzungumza "katika jina la Mungu" ya maanisha kusema kwa nguvu na mamlaka, au kama mwakilishi wake.

ufukufu

Kwa ujumla, neno "utukufu" la maanisha heshima, uzuri, na ukubwa wa ajabu. Chochote chenye utukufu cha semekana kuwa na "utukufu"

sifa

Kumsifu mtu ni kuonyesha matamanio na heshima kwa huyo mtu.

1 Chronicles 16:36

kutoka milele na milele

"milele"

Watu wote

"Watu" au "Kila mtu aliyepo hapo"

1 Chronicles 16:37

kama kazi za kila siku zilivyo itaji

"kama ilivyo itajika kila siku katika sheria ya Musa"

watumike mbele ya hema

"kutumika ndani au karibu na hema ya kukutani"

1 Chronicles 16:40

Walikuwa

"Makuhani"

1 Chronicles 16:42

upatu

Ona ulivyo tafsiri 13:7

1 Chronicles 17

1 Chronicles 17:1

kuwa katika nyumba yake

kuridhika na kuwa na furaha, bila tamanio la kuhama wala kubadilika.

nyumba jengwa na mierezi

Mbao za kutoka kwenye miti ya mierezi ili hesabiwa kuwa mbao bora ya ujenzi.

fanya yalio moyoni mwako

Daudi anaelezwa afanye sawa na sehemu ya mwili yenye hisia. "fanya utakacho taka kufanya"

Mungu yupo nawe

Kuwa katika makubaliano na Mungu ni kama kufanya kazi naye kwasababu Mungu atakusaida kufanikiwa. "Mungu akubaliana na unacho taka kufanya"

1 Chronicles 17:3

neno la Mungu lilimjia

"Mungu alizungumza neno lake"

niliyo ileta Israeli

"kwamba nili waleta Waisraeli kwenye nchi ya ahadi kutoka Misri"

hema, hema la kukusanyikia

Yote haya maneno "hema" na "hema la kukusanyikia" ya eleza kitu kimoja na kutia mkazo kwamba aliishi katika jengo lisilo la kudumu.

Kwa nini haujanijengea mimi nyumba ya mierez?

"Ungenijenga nyumba yenye mbao za gharama."

1 Chronicles 17:7

Nilikuchugua kutoka malishoni

Kazi ya Daudi kama mchungaji ya taja kwa sehemu aliyo chunga kondoo zake. "Nilikutoa kwenye kazi yako kama mchungaji"

malishoni

Ona jinsi ulivyo tafsiri 4:39

1 Chronicles 17:9

Maelezo ya Jumla

Mungu anaendelea kuzungumza ujumbe Nathani anao paswa kumpa Daudi.

nitawapanda hapo

Mungu ana taja kuwaweka Waisraeli kwenye nchi ya ahadi kama mmea aliyo uotesha kwenye ardhi. "Nitawapandikisha hapo"

siku zile nilipo waamuru

Kipindi cha vizazi vingi kina tajwa kama siku. "nilipo amuru" au kutoka vizazi nilivyo amuru"

kuwa juu ya watu wangu Waisraeli

Kuwa katika mamlaka yaelezwa kama kua juu ya mtu. "kuwaamuru watu wangu Israeli"

maadui zako wote ... nina kwambia

Maneno "zako" na "nina kwambia" ya muhusu Daudi.

nitawatiisha

kumfanya mtu au mnyama asiweze kutembea.

nitakujengea nyumba

Yahweh anaeleza kumpa Daudi wazao wengi kutawala juu ya Israeli kama kumjenga nyumba.

1 Chronicles 17:11

siku zako zitapo timia

Maisha yana tajwa kama idadi kadhaa za siku. "utakapo kufa"

kwenda kwa baba zako

Haya maneno yaeleza kifo kama sehemu mababu wa Daudi walipo kwasababu wamekufa tayari.

nitainua uzao wako

Kumueka mtu katika uongozi ya tajwa kama kumuinua juu sana.

nitaimarisha kiti chake cha enzi

Haki ya kutawala kama mfalme imeelezwa kama sehemu ya mfalme kuishi.

1 Chronicles 17:13

na kiti chake cha enzi

Haki ya kutawala kama mfalme imeelezwa kama sehemu ya mfalme kuishi. "na haki yake ya kutawala"

na kumtaarifu

"kumwabia"

1 Chronicles 17:16

akasema

"Daudi akasema"

Mimi ni nani, Yahweh Mungu, na familia yangu ni nini, hadi unilete umbali huu?

Daudi anauliza ili swali kuonyesha shukurani kuwa Mungu amemchagua kumbariki ata kama hastahili.

Hili lilikuwa jambo dogo

Kitu kisicho cha muhimu cha elezwa kuwa kidogo.

machoni pako

Machoni pa Yahweh ya husishwa na ufahamu wake.

Nini zaidi mimi, Daudi, niseme?

Daudi anatumia hili swali kuonyesha kuwa hawezi kueleza kabisa shukrani zake kwa Mungu. "Kama ningeweza sema zaidi kuonyesha shukurani zangu kisha ningefanya lakini sijui nini tena niseme"

mtumishi wako

Daudi anaeleza kuwa yeye ni mtumishi wa Yahweh.

Umemheshimu mtumishi wako. Umemtambua kwa kipekee mtumishi wako

Maneno yote mawili yana maana moja. Kama lugha yako ina maana moja ya kueleza "heshima" na "utambuzi" kisha hii yaweza tafsiriwa kama neno moja.

1 Chronicles 17:19

wa ajili ya mtumishi wako

"faida yangu"

uliwaokoa kutoka Misri

"kuwaokoa kutoka utumwani Misri"

matendo makuu na yahajabu

Maneno "makuu" na "ya ajabu" yana maana moja na kukazia uzito wa ukuu. "matendo mazuri ya ajabu"

1 Chronicles 17:22

itimizwe milele

"iendele milele"

1 Chronicles 17:25

utamjengea nyumba

Kuwa na watoto na kukuza familia kubwa yaelezwa kama kujenga nyumba.

nimepata ujasiri

"kuwa mjasiri wakutosha"

umeibariki, na itabarikiwa milele

Ina maana moja, imerudiwa kwa mkazo.

1 Chronicles 18

1 Chronicles 18:1

Baada ya haya

"Baada ya Mungu kuahidi kumbariki Daudi"

1 Chronicles 18:3

Hadadezeri

Hili ni jina la mwanaume.

Zoba

Hili ni jina la nchi.

magari ya farasi elfu

"magari ya farasi 1000"

wanaume wa farasi elfu saba

Hawa ni wana jeshi walio endesha farasi. "wanaume wa farasi 7000"

wanajeshi wa miguu elfu ishirini

Hawa ni wana jeshi waliyo tembea. "wanajeshi wa miguu 20,000"

aliwajeruhiku

kulemaza mtu au mnyama kwa kumkata msuli wa nyuma ya paja

akahifadhi

kutunza kwa matumiza maalumu

magari ya farasi mia moja

"magari ya farasi 100"

1 Chronicles 18:5

aliua wanaume elfu ishirini na mbili

elfu mbili - "aliua 22,000"

vikosi

kundi la wana jeshi waliyo pangiwa eneo fulani.

1 Chronicles 18:7

Hadadezeri

Ona jinsi ulivyo tafsiri jina lake 18:3

Tibhathi ... Kuni

Haya ni majina ya miji.

saani ya shaba

Hii ni bakuli kubwa ya shaba, kiasi cha mita 5 upana, hiliyo wekwa hekaluni kwa kunawia kipindi cha sherehe.

1 Chronicles 18:9

Toi ... Hadoramu

Haya ni majina ya wanaume

amepigana

"amekuwa katika vita na"

1 Chronicles 18:12

Abishai ... Zeruia

Haya ni majina ya wanaume.

Waedomi elfu kumi na nane

"Waedomi 18,000"

Bonde la Chumvi

Hili ni jina la bonde katika ya Edomu na Yuda uliyo tumika kama uwanja wa pambano.

vikosi

makundi ya wana jeshi yaliyo pangwa sehemu maalumu.

Waedomi wote wakawa watumishi wa Daudi

"watu wa Edomi walilazimishwa kumkubali Daudi kama mfalme na kulipa pesa kwa serikali ya Daudi kila mwaka"

1 Chronicles 18:14

Zeruia ... Ahiludi ... Ahitubi ... Abiathari ... Shavisha ... Benaia ... Yehoiada

Haya ni majina ya wanaume.

mtunza kumbukumbu

mtu anaye fanya kazi ya kuandika maelezo ya maalumu ya matukio.

Ahimeleki

Hili jina linawakilisha sahisho la "Abimeleki," ambalo tafsiri zingine zinatumia. Sahisho hili linafanya huu mstari ukubaliane na 8:15.

Zadoki mwana wa Ahitubi na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani

Baadhi ya tafsiri ina sahisha hili kusema kwamba Ahitubi na Ahimeleki walikuwa makuhani wa kuu.

Wakerethi ... Wapelethi

Haya ni majina ya makundi ya watu.

1 Chronicles 19

1 Chronicles 19:1

Nahashi ... Hanuni

Haya ni majina ya wanaume.

Nitaonyesha ukarimu ... alionyesha ukarimu

"Nitakuwa mkarimu ... alikuwa mkarimu"

kumfariji

"kuliwaza"

Unadhani Daudi anamheshimu baba yako sababu ametuma watu kukufaraji?

"Usidhani kuwa Daudi ana muheshimu baba yako kwasababu ametuma wanaume kukufariji."

Je watumishi wake hawajaja kutadhimini nchi iliwaipindue?

"Hakika watumishi wanakuja kwako kudadisi nchi ili waipindue."

1 Chronicles 19:4

mavazi

"nguo"

alienda kukutana nao

"alituma wajumbe kwenda kuwafariji"

walifedheeka sana

Fedhea yaelezewa kubwa sana kuonyesha jinsi ilivyo wahadhiri. "aibika sana"

1 Chronicles 19:6

wamekuwa kikwazo kwa Daudi

Neno "uvundo" la elezea harafu mbaya. Hii yaelezea Waamoni kama kitu kibaya na hakitakiwi.

talanta elfu moja

"talanta 1,000"

Naharaimu .. Maka ... Zoba ... Medeba

Haya ni majina ya miji.

1 Chronicles 19:8

alipo sikia

"alisikia Waamoni walikuwa wanakuja kwa vita"

kukutana nao

"kupigana dhidi yao"

1 Chronicles 19:10

Abishai

Hili ni jina la kaka wa Yoabu.

1 Chronicles 19:12

Kuwa thabiti

"Kuwa shupavu"

natujionyeshe kwa watu wetu kuwa ni wenye nguvu

"tutende kwa ujasiri"

1 Chronicles 19:14

wasogea kwenye pambano

"alienda mbele kwenye pambano" au "aliwafuata maadui wana jeshi kwenye pambano"

1 Chronicles 19:16

Waaremi walipoona

"Waaremi walielewa"

msaada

"wana jeshi zaidi"

Shofaki ... Hadadezeri

Haya ni majina ya wanaume.

Daudi alipo ambiwa haya

Wajumbe wake walipo mwambia Daudi hili.

Alipanga

"kuweka vizuri"

wakapigana nao

"Waaremi wakapigana na Daudi na wana jeshi wake"

1 Chronicles 19:18

akaua elfu saba

"akaua 7,000"

wanajeshi wa miguu elfu arobaini

wanajeshi wa miguu 40,000"

Shofaki ... Hadadezeri

Haya ni majina ya wanaume.

1 Chronicles 20

1 Chronicles 20:1

kusikitisha nchi

"kuharibu nchi" Hii yaeleza jeshi linapo haribu nchi maadui zao wanapo otesha chakula

1 Chronicles 20:2

Taji liliwekwa kichwani mwa Daudi

"Wanaume wa Daudi wakaeka taji kichwani kwake"

akaleta mali

vitu vya thamani vilivyo chukuliwa vitani.

Daudi aliwataka watu wote wa mji

Watu wanatajwa kwa miji yao. "Daudi aliwataka watu wote wa miji"

1 Chronicles 20:4

Gezeri ... Gobu

Haya ni majina ya miji

Sibekai ... Sipai ... Elhanani ... Lahmi

Haya ni majina ya wanaume.

Mhushathi ... Refaimu ... Mbethilehemu ... Mgiti

Haya ni majina ya makundi ya watu.

wakazidiwa

kumtawala mtu au kitu kwa kutumia nguvu.

gongo

mbao ndefu na nyembamba

gongo la mshonaji

aina ya mbao inayo tumika kunyoosha mapindo wakati nyuzi za zuria zinashonwa pamoja kuzunguka.

1 Chronicles 20:6

Refaimu

Hilo ni jina lililo pewa jamii ya watu ambao walikuwa warefu na imara.

Yehonadabu ... Shimea

Haya ni majina ya wanaume.

waliuawa na mkono wa Daudi na mkono wa wanajeshi wake

Daudi na wana jeshi wake wana tajwa kwa sehemu ya miili yao inayo tumika kushikilia upanga. "Daudi na wana jeshi wake waliua wazao wa Refaimu"

1 Chronicles 21

1 Chronicles 21:1

Adui akainuka dhidi ya Israeli

Kuwa juu kunafafanua kuwa na nguvu zaidi. "'Adui wa Israel walikuwa na nguzu zaidi"

Kumchochea

Kumsababisha mtu afanye kitu.

Kutoka Beerisheba mpaka Dani

Waisraeli waliichukulia hii miji miwili miji yao ya kusini zaidi na kaskazini zaidi. Daudi alitumia hii miji miwili kufikia Waisraeli wote.

Mara mia zaidi ya lilivyo

Yoabu alieleza matamanio ya kuwa na jeshi lenye ukubwa wa watu 100 kwa kusema angependa jeshi liwe na wanajeshi zaidi na lenye nguvu.

Lakini bwana wangu mfalme, kwani wote hawamtumikii bwana wangu? kwanini bwana wangu anataka hili? Kwanini ulete hatia kwa Israeli?

Lakini bwana wangu mfalme, wote wanakutumikia tayari. Bwana wangu asiombe hili. Utaleta tu hatia kwa watu wa Israeli kwa matamanio yako ya nguvu ya kijeshi.''

Kwanini bwana wangu analitaka hili?

Neno ''hili'' limemaanisha mpango wa Daudi kuhesabu wanaume waote wa Israeli.

1 Chronicles 21:4

Neno la mfalme halikubadilika

Mstari huu wahusu amri ya mfalme Daudi kuwa ya mwisho kwasababu hatabadili amri yake baada ya kuitoa. "amri ya mfalme haitakuja kubadilika"

wanaume waliobeba upanga

Maaskari wa Israeli walielezewa kwa kitendo cha kuvuta upanga na kupigana nao.

1 Chronicles 21:6

Lakini Levi na Benjamini hawakus hesabiwa miongoni mwao

" Lakini Yoabu hakuwa hesabu wanaume kutoka makabila ya Levi na Benjaminini"

kwa hili tendo

"tendo hili" limemaanisha katika mpango wa Daudi kuhesabu wanaume wote wa Israeli wenye uwezo wa kupigana.

chukua hatia ya mtumishi wako

Msamaha unafafanuliwa kama kuwa na hatia halafu ikaondolewa. "Nisamehe mimi"

hatia ya mtumishi wako

Daudi anajitaja mwenyewe kama mtumishi wa Mungu. "hatia yangu"

1 Chronicles 21:9

Yahweh

Neno "Yahweh" ni jina binafsi la Mungu ambalo alilidhihirisha alipokuwa anazungumza na Musa kwenye kichaka cha moto.

Gadi

Gadi ni moja ya wana wa Yakobo, ambaye ni, Israeli.

nabii, unabii, kutoa unabii, muonaji, nabii wa kike

"nabii" ni mwanaume anaye ongea jumbe za Mungu kwa watu. Mwanamke anaye fanya haya anaitwa "nabii wa kike"

1 Chronicles 21:11

kupatwa na upanga wao

Haya maneno ni namna nyepesi ya kueleza kuuliwa na adui.

kupatwa na upanga wao

Haya maneno ni eleza mbinu ya Yahweh ya kuua kwa kifaa mwanajeshi angetumia kuua.

akiharibu

"akiua"

1 Chronicles 21:13

Nipo katika shida kubwa

"Nipo kwenye shida nyingi"

Acha nianguke katika mikono ya Yahweh kuliko kuangukia mikono ya mwanadamu, sababu matendo yake ya rehema ni makubwa mno

"Acha nije katika utawala wa Yahweh, kuiko chini ya utawala wa watu, kwa kuwa Yahweh ni wa rehema sana"

na watu elfu sabini wakafa

"na watu 70,000 wakafa"

kubadili nia yake

Kubadili uamuzi.

Rudisha mkono wako

Yahweh ana mwambia malaika wa uharibifu kuacha kuua watu.

malaika wa Yahweh alikua amesimama

Malaika wa Yahweh anaelezwa kama kitu kilicho simama kama mtu anavyo simama.

Orinani

Hili ni jina la mwanaume.

1 Chronicles 21:16

akiwa na upanga mkonono mwake

"tayari kushambulia"

Sio mimi niliye amuru jeshi kuhesabiwa?

"Mimi ndiye niliye amuru jeshi lihesabiwe"

Lakini hawa kondoo

Daudi anawaelezea watu wa Israeli kama aina ya wanyama watao muamini na kumfuata kiongozi.

wamefanya nini?

"Hawaja fanya kitu kinacho stahili adhabu"

1 Chronicles 21:18

Orinani

Ona jinsi ulivyo tafsiri hili jina 21:3

kama Gadi alivyo muelekeza cha kufanya kwa jina la Yahweh

"kama Gadi, akizungumza na mamlaka ya Yahweh, alivyo muambia Daudi afanye"

1 Chronicles 21:21

uso wake ukiwa kwenye ardhi

Haya maneno yaeleza kwamba Orinani aliinama mbele zaidi. Kuina mbele za mtu ni njia ya kuonyesha unyenyekevu na heshima. Kuinama zaidi ya onyesha unyenyekevu mkubwa na heshima.

gharama yote

"Nitalipa gharama yote hili eneo la kupeta lina gharimu"

1 Chronicles 21:23

Chukuwa kama lako

"Chukuwa kama zawadi"

linalo kupendeza

Ufahamu wa Daudi waelezwa kama macho yake. "linalo onekana zuri kwako"

vifaa vya kupeta

kifaa cha mbao na mawe au machuma yaliyo wekwa kwa chini, inatumika kugawa mbegu kutoka kwenye maganda kwa kuvuta juu unga ulioekwa chini.

1 Chronicles 21:25

shekeli mia sita ya dhahabu

"shekeli 600 ya dhahabu"

Akamuita Yahweh

"aliomba kwa Yahweh msaada"

malaika akarudisha upanga kwenye mfuko wake

malaika aliacha kuua watu"

mfuko

mfuniko wa upanga au kisu

1 Chronicles 21:28

Orinani

Ona jinsi ulivyo tafsiri jina lake 21:13

Mungu muelekeo

Mungu amwabie ni afanye"

anaogopa upanga wa malaika wa Yahweh.

"anaoga atauliwa na malaika wa Yahweh"

1 Chronicles 22

1 Chronicles 22:1

wachonga mawe,

Hawa ni watu wanao kusanya mawe makubwa na kuyakata katika kipimo sahihi ili wa jenzi waeze kutumia mawe kwenye kuta na majeng.

1 Chronicles 22:3

zaidi ya kipimo

"kuliko mtu yeyote awezavyo kupima"

nyumba itayo jengwa kwa Yahweh

"nyumva ya Yahweh" au "nyumba atakayo mjengea Yahweh"

1 Chronicles 22:6

kuitwa

"Daudi aliita"

kumuamuru ajenge ... dhamira yangu kujenga

"aliwaamuru wafanya kazi kujenga ... mpango wangu ulikuwa kuajiri wafanya kazi kujenga"

kwa ajili ya jina la Yahweh Mungu wangu

"kumheshimu Yahweh Mungu wangu"

umemwaga damu nyingi

"umeua watu wengi"

Hauta jenga nyumba kwa jina langu

"Hauta jenga hekalu kunitukuza mimi"

kwasababu umemwaga damu nyingi kwenye ardhi machoni pangu

"kwasbabu ninajua umeua watu wengi"

1 Chronicles 22:9

Maelezo ya Jumla

Daudi anaendelea kumuambia Sulemani kile Yahweh alicho mwambia.

kila upande

Hii ina maana ya kila sehemu kuzunguka Israeli.

katika siku zake

"wakati akitawala Israeli yote"

nyumba kwa jina langu, na nitakuwa baba yake

"hekalu la kunitukuza"

Ata kuwa mwana wangu

Mungu ata mtendea Sulemani kama alikuwa ni mwanae wa pekee.

Nitaimarisha kiti cha enzi cha ufalme wake juu ya Israeli

Hapa "kiti cha enzi" cha husu mamlaka ya kutawala kama mfalme. "Nitafanya uzao wake utawale juu ya Israeli milele"

1 Chronicles 22:11

Maelezo ya Jumla

Daudi anaendelea kuzungumza na Sulemani.

Sasa

Daudi anatumia hili neno kutambulisha kitu muhimu anacho kwenda kusema.

Uweze kujenga

"Uweze kufanikiwa kuelekeza jengo"

ata kapokuweka kiongozi juu ya Israeli

"atakapo kufanya mfalme juu ya Israeli"

1 Chronicles 22:14

Maelezo ya Jumla

Daudi anaendelea kusema na Sulemani.

Ona

Daudi anatumia hili neno kutambulisha kitu muhimu anacho kwenda kusema

talanta

talanta ni kipimo cha uzito. Kinauzito wa kilogramu 33

milioni moja

"1,000,000"

1 Chronicles 22:15

Maelezo ya jumla

Daudi anaendelea kusema na Sulemani.

wachonga mawe

Hawa ni wafanya kazi ambao wanakata mawe na kuandaa kwa ajili ya wajenzi wa kuta na majengo.

maseremala

Hawa ni watu wanao fanya kazi na mbao.

1 Chronicles 22:17

wenu ... nanyi

Yaeleza wingi 22:18-19

amewapa amani kila pande

"amewaopa amani kutoka vitani kila sehemu ya Israeli"

Amewakabidhi mikononi mwangu wenyeji wote mkoa

"Amenipa nguvu juu ya kila mtu anayeishi kwetu"

Mkoa umetiishwa mbele za Yahweh na watu wake

"Yahweh na watu wake wanatawala nchi"

Sasa

Hili neno la tambulisha kitu muhimu Daudi anachoenda kusema.

mtafuteni Yahweh Mungu wenu

"jaribu kumfanya Yahweh Mungu wenu kuwasikiliza"

kwa moyo wenu wote na nafsi

"kwa dhati" au "moyo wote"

Simameni na mjenge sehemu takatifu

"Simameni na muwaelekeze wafanya kazi wanapo jenga sehemu takatifu"

nyumba iliyo jengwa kwa ajili ya jina la Yahweh

"hekalu utakalo jenga kumheshimu Yahweh"

1 Chronicles 23

1 Chronicles 23:1

Maelezo ya Jumla

Daudi anamteua Sulemani kama mrithi wake na anapanga makuhani wa Kiwalawi na wafanya kazi wa huduma za hekaluni

Walawi walio kuwa miaka thelathini na zaidi walihesabiwa

"Baadhi ya wanaume wa Daudi waliwahesabu Walawi walikuwa na miaka 30 na zaidi"

Idadi ya elfu thelathini na nane

elfu nane "Walikuwa 38,000"

1 Chronicles 23:4

Kwa hawa, elfu ishirini na nne

elfu nne "Kwa hawa Walawi, 24,000"

elfu sita

"Walawi 6,000"

maaskari na waamuzi

Hawa Walawi walisikiliza mashtaka ya kisheria na kutoa haki kwa mujibu wa sheria ya Musa.

Elfu nne

"Walawi 4,000

walinzi wa lango

Hawa Walawi walilinda lango ili mtu najisi hasiingie"

kulingana

"kwa mujibu wa" au "kwa uzao wa"

Gerishoni, Kohathi, na Merari

Haya ni majina ya wana wa Walawi.

1 Chronicles 23:7

Maelezo ya Jumla

Haya ni majina ya Walawi kulingana na koo zao.

1 Chronicles 23:10

Maelezo ya Jumla

Hii yaendeleza orodha ya Walawi kwa mujibu wa koo zao.

hivyo walihesabiwa kama ukoo mmoja

"hivyo Daudi akawahesabu kama koo moja"

1 Chronicles 23:12

Maelezo ya Jumla

Hii yaendeleza orodha ya Walawi kwa mujibu wa koo zao.

Palikuwa na wanne wa wana wa Kohathi

"Kohathi alikuwa na wana 4"

Aruni alichaguliwa kuandaa vitu vitakatifu

"Yahweh alimchagua Aruni kuvitoa vitu vitakatifu"

kumpa baraka kwa jina lake

"kuwa bariki watu kama wa wakilishi wa Mungu milele"

wana wake walihesabiwa kuwa Walawi

"wana wake walikuwa sehemu ya ukoo wa Walawi" Wana wa Musa walikuwa Walawi.

1 Chronicles 23:15

Maelezo ya Jumla

Hii yaendeleza orodha ya Walawi kwa mujibu wa koo zao

1 Chronicles 23:19

Maelezo ya Jumla

Hii yaendeleza orodha ya Walawi kwa mujibu wa koo zao

1 Chronicles 23:21

Maelezo ya Jumla

Hii yaendeleza orodha ya Walawi kwa mujibu wa koo zao

1 Chronicles 23:24

Hawa walikuwa uzao wa Lawi kuligana na koo zao. Walikuwa viongozi, wamehesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, kuanzia koo

"Haya yalikuwa majina ya uzao wa Lawi na familia zao, ambao Daudi aliwahesabu na kuwaorodhesha. Walikuwa viongozi wa koo"

kutoka miaka ishirini na zaidi

"kutoka miaka 20 na zaidi"

na vifaa vyake vinavyo tumika kwenye utumishi wake

"na vifaa vyake walivyo tumia kwenye utumishi wake"

1 Chronicles 23:27

Kwa maneno ya Daudi ya mwisho Walawi walihesabiwa

"Amri ya Daudi ya mwisho ilikuwa wanaume wake wa wahesabu walawi"

miaka ishirini na kuendelea

"walio kuwa miaka 20 na kuendelea"

mkate wa uwepo

Ona jinsi ulivyo tafsiri 9:30

unga

unga mtu anaoupata kwa kusaga mbegu

sadaka ziliochanganywa na mafuta

"sadaka mtu alizozichanganywa na mafuta

1 Chronicles 23:30

Pia walisimama

"Walawi Pia walisimama"

na kila wakati sadaka ya kuteketezwa ilipo tolewa kwa Yahweh

"wakati makuhani walipo toa sadaka ya kuteketezwa kwa Yahweh"

sherehe za mwezi mpya

Hizi siku kuu ziliadhimisha mwanzo wa kila mwezi.

Idadi iliyo pangwa, iliyo tolewa kwa amri, ilipaswa kuwa mbele ya Yahweh

"Ilikuwa ni wajibu wa baadhi ya idadi ya watu wa Walawi kuwepo wakati wa kutoa sadaka kwa Yahweh"

1 Chronicles 24

1 Chronicles 24:1

Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari

Ona jinsi ulivyo tafsiri haya majina 6:1

Ahimeleki

Hili ni jina la mwanaume.

waliwagawanya katika makundi

"aliwagawanya wazao wa Eleazari na Ithamari kwenye makundi"

1 Chronicles 24:4

waligawanya

"Daudi, Zadoki, na Ahimeleki waligawanya"

makundi kumi na sita

"makundi 16"

Magawanyo haya yalikuwa nane kwa idadi

"Walikuwa na magawanyo 8 kulingana na koo za uzao wa Ithamari"

1 Chronicles 24:6

Shemaia

Hili ni jina la mwanamume.

Nethaneli

Ona jinsi ulivyo tafsiri 15:22

Ahimeleki

Ona jinsi ulivyo tafsiri 18:14

Ukoo mmoja ulichaguliwa kwa kura kutoka uzao wa Eleazari, na kisha uliofata utachaguliwa kutoka uzao wa Ithhamari

"Walimchagua mmoja kwa kura kutoka uzao wa Eleazari, kisha watachagua kwa kura kutoka uzao wa Ithamari"

1 Chronicles 24:7

Maelezo ya Jumla

Hii ni utaratibu wa huduma ambao Daudi, Zadoki, na Ahimeleki walichagua kwa orodha kwa uzao wa Eleazari na Ithamari.

1 Chronicles 24:11

Maelezo ya Jumla

Hii ni utaratibu wa huduma ambao Daudi, Zadoki, na Ahimeleki walichagua kwa orodha kwa uzao wa Eleazari na Ithamari.

1 Chronicles 24:15

Maelezo ya Jumla

Hii ya hitimisha utaratibu wa huduma ambao Daudi, Zadoki, na Ahimeleki alichagua kwa kura kwa uzao wa Eleazari na Ithamari.

1 Chronicles 24:19

wakifuata utaratibu waliopewa na Aruni babu yao

"wakifuata sheria ambazo Aruni babu yao aliwapa"

1 Chronicles 24:20

Maelezo ya Jumla

Hii inaanza orodha ya majina ya wana wengine wa Lawi. orodha itaisha 24:29

Amramu

Ona jinsi ulivyo tafsiri 6:1

Shebueli

Ona jinsi ulivyo tafsiri 2315

1 Chronicles 24:23

Hebroni ... Yeria ... Amaria ... Yahazieli ... Yekameamu

Ona jinsi ulivyo tafsiri 23:19

Uzieli ... Mika ... Ishia

Ona jinsi ulivyo tafsiri 23:19

Shamiri ... Zakaria

Haya ni majina ya wanaume.

1 Chronicles 24:26

Merari ... Mahli ... Mushi ... Eleazari

Ona jinsi ulivyo tafsiri 23:21

Yaazia, Beno, Shohamu, Zakuri ... Ibrri

Haya ni majina ya wanaume.

1 Chronicles 24:29

Kishi ... Mushi

Ona jinsi ulivyo tafsiri 23:21

Yerameli .. Mahli ... Ederi ... Yerimothi

Haya ni majina ya wanaume.

Ahimeleki

Ona jinsi ulivyo tafsiri 18:14

1 Chronicles 25

1 Chronicles 25:1

Upatu

Ona jinsi ulivyo tafsiri 13:7

Hemani ... Yeduthuni

Ona jinsi ulivyo tafsiri 16:40

Zakuri ... Matithia

Haya ni majina ya wanaume.

sita kwa jumla

"6 kwa jumla"

1 Chronicles 25:4

Maelezo ya Jumla

Hii inaendeleza orodha ya viongozi wa kazi ya hema la kukutania imeanza 25:1

Bukia ... Mahaziothi

Haya ni majina ya wanaume.

Hemani

Ona jinsi ulivyo tafsiri 16:40

wana kumi na nne na mabinti watatu

"wana 14 na mabinti 3"

1 Chronicles 25:6

upatu

Ona jinsi ulivyo tafsiri 13:7

Yeduthuni ... Hemani

Ona jinsi ulivyo tafsiri 16:40

idadi ya 288

"walikuwa wanaume mia mbili na themanini na nane"

sawa kwa vijana na kwa wazee, kwa walimua na kwa wanafunzi

Hii yaeleza mkazo "wote hao"

1 Chronicles 25:9

Maelezo ya Jumla

Hii yaanza orodha ya kura 24 zilizo tupwa kuchagua utaratibu za familia gani zitakazo hudumu. Hii orodha yaisha 25:29

ya kwanza ... ya pili

Hii yaonyesha utaratibu wa familia zilizo chaguliwa. "namba 1 ...namba 2 ... namba 3 ... namba 4 ... namba 5" au tumia " wa awali" kwa "wa kwanza" na "akifuatiwa" kwa wote wano fuata.

kura ya kwanza iliangukia katika familia ya Yusufu

Kwa watu wote kwenye orodha, nakala ya eleza kwamba palikuwa "watu kumi na mbili kwa idadi" Kwa maana hii imegusiwa, unaweza ongeza hii sentensi kwa ajili ya Yusufu, kama UDB inavyo fanya. "kura ya kwanza ilimwangukia familia ya Yusufu, watu kumi na mbili kwa idadi"

Yusufu ... Zakuri ... Nethania

Ona jinsi ulivyo tafsiri haya majina 25:1

Gedalia

Ona jinsi ulivyo tafsiri haya majina 25:1

watu kumi na mbili

"watu 12"

Izri

Hili jina limeandikwa Zeri 25:1

1 Chronicles 25:13

Maelezo ya Jumla

Hii ya endeleza orodha iliyo anzishwa 25:9

ya sita ... ya tisa

Hii ya onyesha utaratibu jinsi familia zilivyo chaguliwa. "namba 6" ... namba 7 ... namba 8 ... namba 9"

Bukia

Ona jinsi ulivyo tafsiri 25:4

watu kumina mbili

"watu 12"

Yesharela

Aina nyingine ya kuandika "Ashareka" 25:1

Yeshaia

Ona jinsi ulivyo tafsiri 25:1

Matania

Ona jinsi ulivyo tafsiri 25:4

1 Chronicles 25:17

Maelezo ya Jumla

Hii yaendeleza orodha iliyo anzwa 25:9

ya kumi ... ya kumi na tatu

Hii ya onyesha orodha jinsi familia zilivyo chagulliwa. "namba 10 ... namba 11 ... namba 13"

Shimei

Ona jinsi ulivyo tafsiri 25:1

watu kumi na mbili

"watu 12"

Azareli

Hii ni aina nyingine ya kuandika "Uzieli" 25:4

Hashabia

Ona jinsi ulivyo tafsiri 25:1

Shubaeli

Ona jinsi ulivyo tafsiri 25:4

1 Chronicles 25:21

Maelezo ya Jumla

Hii yaendeleza orodha iliyo anzwa 25:9

ya kumi na nne ... kumi na saba

Hii yaonyesha utaratibu familia zilivyo chaguliwa. "namba 14 ... namba 15 ... namba 16 ... namba 17"

Matithia

Ona jinsi ulivyo tafsiri 25:1

watu kumi na mbili

"watu 12"

Yeremothi

Hii ni aina nyingine ya kuandika "Uzieli" 25:4

Hanania

Ona jinsi ulivyo tafsiri 25:4

Yoshibekasha

Ona jinsi ulivyo tafsiri 25:4

1 Chronicles 25:25

Maelezo ya Jumla

Hii yaendeleza orodha iliyo anza 25:9

ya kumi na nane ... ishirini na moja

kwanza Hii yaonyesha utaratibu wa familia zilizo chaguliwa. "namba 18 ... namba 19 ... namba 20 ... namba 21"

Hanani

Ona jinsi ulivyo tafsiri 25:4

watu kumi na mbili

"watu 12"

Malothi

Ona jinsi ulivyo tafsiri 25:4

Eliatha

Ona jinsi ulivyo tafsiri 25:4

Hothiri

Ona jinsi ulivyo tafsiri 25:4

1 Chronicles 25:29

Maelezi ya Jumla

Hii ya hitimisha orodha illiyo anza 25:9

ya ishirini na mbili ... ya ishirini na nne

ya pili ... ishiri na nne Hii yaonyesha utaratibu wa jinsi familia zilivyo chaguliwa. "namba 22 ... namba 23 ... namba 24"

Gidalti

Ona jinsi ulivyo tafsiri 25:4

watu kumi na mbili

"watu 12"

Mahaziothi

Ona jinsi ulivyo tafsiri 25:4

Romamti Eza

Ona jinsi ulivyo tafsiri 25:4

1 Chronicles 26

1 Chronicles 26:1

Maelezo ya Jumla

Hii yaanza orodha ya walinzi wa lango

Wakora

Ona jinsi ulivyo tafsiri 9:17

Meshelemia

Ona jinsi ulivyo tafsiri 9:20

Kore

Ona jinsi ulivyo tafsiri 9:17

Asafu

Hili ni jina mbadala la "Ebiasafu" 9:17

Zekaria

Ona jinsi ulivyo tafsiri 9:20

Yediali ... Zebadia ... Yathnieli ... Elamu ... Yehonani ... Eliehoenai

Haya ni majina ya wanaume

wa pili ... watatu ... ya nne ... wa saba

Hii yaonyesha utaratibu ya wana kuzaliwa. "namba 2 ... namba 3 ... namba 4 ... namba 7" au "afuatae" kwa kila mmoja.

1 Chronicles 26:4

Maelezo ya Jumla

Hii yaendeleza orodha ya walinzi wa lango iliyoanza

Obedi Edomu

Ona jinsi ulivyo tafsiri 9:37

Shemaia ... Yehozabadi ... Yoa ... Sakari ... Nethanieli ... Amieli ... Isakari ... Peulethai

Haya ni majina ya wanaume.

wapili ... wanane

Hii yaonyesha utaratibu jinsi wana walivyo zaliwa. "namba 2 ... namba 3 ... namba 4 ... namba 5 ... namba 6 ... namba 7 ... namba 8 au "afuatae" kwa kila moja.

1 Chronicles 26:7

Maelezo ya Jumla

Hii yaendeleza orodha ya walinzi wa lango iliyo anza

Shemaia ... Obedi Edomu

Ona jinsi ulivyo tafsiri 26:4

ndugu zake

" ndugu wa Shemaia" au "ndugu wa familia ya Shemaia"

Othini, Refaeli, Obedi ... Elizabadi ... Elihu ... Semakia ...

Haya ni majina ya Wanaume.

sitini na mbili

wawili "wanaume 62"

jumla ya kumi na nane

"jumla 18"

1 Chronicles 26:10

Maelezo ya Jumla

Hii inaendeleza orodha ya walinzi wa lango iliyo anza

Hosa ... Merari ... Shimiri ... Hilika ... Tebalia ... Zekaria

Haya ni majina ya wanaume.

wa pili ... watatu ... wanne

Hii yaonyesha utaratibu wana walivyo zaliwa. "namba 2 ... namba 3 ... namba 4" au "anaefuata" kwa kila moja.

Wote wa wana wa Hosa na ndugu walikuwa kumi na tatu kwa idadi

"Hawa walikuwa wana 13 wa Hosa na ndugu zake"

1 Chronicles 26:12

wadogo kwa wakubwa

"kila mtu" au "wanaume wa miaka yote"

Shelemeia

Hii ni aina nyingine kuandika "Meshelemia" 26:1

Zekaria

Ona jinsi ulivyo tafsiri 26:1

Kura ilipo rushwa

"Walipo rusha kura"

mshauri makini

Huyu ni mtu anaye onyesha hukumu nzuri katika kufanya maamuzi.

1 Chronicles 26:15

Obedi Edomu kulipangiwa lango la kusini, na wanae walipangiwa nyumba za ghala

"Obedi Edomu ilikuwa na wajibu wakulinda lango la kusini, na wana wake walilinda nyumba za ghala"

Obedi Edomu

Ona jinsi ulivyo tafsiri 26:4

Shupimu

Hili ni jina la mwanamume

Hosa

Ona jinsi ulivyo tafsiri 26:10

Shalekethi

Hilil ni jina la lango.

Lindo lilikabiidhiwa kwa kila familia.

"Kila familia ilikuwa na wajibu wakulinda kitu"

1 Chronicles 26:17

Walawi sita

"Walawi 6"

wanne walipangwa

"wanaume 4 kila siku"

wawili

"wanaume wa 2" au "wanaume 2 kwa zamu"

Katika ua kuelekea magharibi wanne walipangwa

"wanaume wa 4 walilinda ua la magharibi"

wanne barabarani, na wawili katika ua

Wanaume wa 4 walilinda barabara, na wanaume wawili walilinda ua"

Palijazwa na

"Walikuwa"

Merari

Ona jinsi ulivyo tasfiri 26:10

1 Chronicles 26:20

Wazao wa Ladani, walitoka kwa Gerishoni kupitia kwake na walio kuwa viongozi wa familia za Ladani Mgerishoni, walikuwa Yehieli na wanae

"Yehieli na wanae walikuwa uzao wa Ladani, aliye toka Gerishoni ulio wa Ladani. Yehieli na wana wake walikuwa viongozi wa familia ya Ladani Mgerishoni. Wana wa Yehieli"

Ladani ... Gerishoni

Ona jinsi ulivyo tafsiri haya majina 23:7

Mgerishoni

Wazao wa Gerishoni.

Yehieli ... Zethamu ... Yoeli

Ona jinsi jinsi ulivyo tafsiri haya majina katika 23:7.

aliyesimamia

"aliye kuwa msimamizi"

1 Chronicles 26:23

Kulikuwa na askari walio chukuliwa kwa koo

"Viongozi walichagua askari kutoka koo"

Amramu, Izhari, Hebroni, Uzieli

Ona jinsi ulivyo tafsiri haya majina 23:12

Shebueli ... Gerishomu ... Eliezeri ... Rehabia

Ona jinsi ulivyo tafsiri haya majina 23:15

Yeshaia ... Yoramu ... Zikiri Shelomothi

Haya ni majina ya wanaume.

1 Chronicles 26:26

maelfu na mamia

"zaidi ya wanaume 1,000 na zaidi ya wanaume 100"

vitu walivyo vichukuwa

vitu jeshi linavyo chukuwa baada ya ushindi

Kishi ... Neri ... Zeruia

Haya ni majina ya wanaume

Kila kitu kilicho tengwa

"vitu vyote viongozi walivyo vitenga"

1 Chronicles 26:29

Izhari ... Hebroni

Ona jinsi ulivyo tafsiri haya majina 23:12

mambo ya ndani ya Israeli

Hii ya husu shughuli za watu wa Israeli, haya uhusiano na jeshi wala hekalu. "shughuli za watu wa Israeli"

Kenania ... Hashabia

Haya ni majina ya wanaume.

wanaume wenye uwezo 1,700

"wanaume elfu moja na mia saba wenye uwezo"

kazi ya Yahweh na kazi ya mfalme

"kazi iliyo fanywa ya Yahweh na mfalme"

1 Chronicles 26:31

Hebroni

Ona jinsi ulivyo tafsiri 23:12

Yerija

Namna nyingine ya kuandika "Yeria." Ona jinsi ulivyo tafsiri 23:19

walihesabiwa kutoka orodha

"majina yao yalikuwa kwenye orodha"

Katika mwaka wa arobaini wa utawala wa Daudi

"Daudi alipo kuwa mfalme kwa miaka 40"

Yazeri

Hili ni jina la mwanaume.

ndugu 2,700

"elfu mbili na mia saba ndugu"

1 Chronicles 27

1 Chronicles 27:1

Hii ni orodha

"Haya ni majina"

namna tofauti

"namna za tofauti" au "njia nyingi"

Kila kikosi cha jeshi

"Kila kundi"

wanaume elfu ishirini na nne

wanaume elfu nne "wanaume 24,000"

mwaka mzima

"mwaka wote"

mwezi wa kwanza

Huu ni mwezi wa kwanza wa kalenda ya Kiebrania. Ni wakati wa mwisho wa Machi na mwanzo wa Aprili kwa kalenda za Kimagharibi.

Yashobeamu mwana wa Zabdieli

Haya ni majina ya wanaume.

mhusika

"kiongozi"

1 Chronicles 27:4

mwezi wa pili

Huu ni mwezi wa pili wa kalenda ya Kiebrania. Ni wakati wa mwisho wa Aprili na mwanzo wa Mei kwa kalenda za Kimagharibi.

Dodai ... Amizabadi

Haya ni majina ya wanaume.

kikosi chake

"katika kundi lake la jeshi" au kundi la wanajeshi wake"

wanaume elfu ishirini na nne

wanaume elfu nne "wanaume 24,000"

mwezi wa tatu

Huu ni mwezi wa tatu wa kalenda ya Kiebrania. Ni wakati wa mwisho wa Mei na mwanzo wa Juni kwa kalenda za Kimagharibi.

wale thelathini

Ona jinsi ulivyo tafsiri 11:10

1 Chronicles 27:7

Mkuu kwa mwezi wa nne alikuwa Asaheli kaka wa Yoabu

"Asaheli, kaka wa Yoabu, alikuwa mkuu wa mwezi wa nne"

mwezi wa nne

Huu ni mwezi wa nne wa kalenda ya Kiebrania. Ni wakati wa mwisho wa Juni na mwanzo wa Julai kwa kalenda za Kimagharibi.

Asaheli ... Ikeshi

Haya ni majina ya wanaume.

kikosi chake

"kundi lake la jeshi"

wanaume elfu ishirini na nne

wanaume elfu nne "wanaume 24,000"

mwezi wa tano

Huu ni mwezi wa tano wa kalenda ya Kiebrania. Ni wakati wa mwisho wa Julai na mwanzo wa Agusti kwa kalenda za Kimagharibi.

mwezi wa sita

Huu ni mwezi wa sita wa kalenda ya Kiebrania. Ni wakati wa mwisho wa Agusti na mwanzo wa Septemba kwa kalenda za Kimagharibi.

Tekoa

Hili ni jina la sehemu.

1 Chronicles 27:10

Mkuu kwa mwezi wa saba alikuwa Helezi Mpeloni, kutoka watu wa Efraimu

"Helezi, Mpeloni, kutoka watu wa Efraimu, alikuwa mkuu wa mwezi wa saba"

mwezi wa saba

Huu ni mwezi wa saba wa kalenda ya Kiebrania. Ni wakati wa mwisho wa Septemba na mwanzo wa Oktoba kwa kalenda za Kimagharibi.

Helezi ... Sibekai ... Zera ... Abi Ezeri

Haya ni majina ya wanaume.

Mpeloni ... Mhushathi ... Manathothi

Haya ni majinaya makabila au koo.

wanaume elfu ishirini na nne

wanaume ekfu nne "wanaume 24,000"

mwezi wa nane

Huu ni mwezi wa nane wa kalenda ya Kiebrania. Ni wakati wa mwisho wa Oktoba na mwanzo wa Novemba kwa kalenda za Kimagharibi.

mwezi wa tisa

Huu ni mwezi wa tisa wa kalenda ya Kiebrania. Ni wakati wa mwisho wa Novemba na mwanzo wa Desemba kwa kalenda za Kimagharibi.

1 Chronicles 27:13

Maharai ... Zera ... Heldai ... Othnieli

Haya ni majina ya wanaume.

mwezi wa kumi

Huu ni mwezi wa kumi wa kalenda ya Kiebrania.

Netofa ... Pirathoni

Haya ni majina ya sehemu. Ni wakati wa mwisho wa mwezi Desemba na mwanzo wa mwezi Januari katika kalenda za Magharibi.

wanaume elfu ishirini na nne

wanaume elfu nne "wanaume24,000"

mwezi wa kumi na moja

Huu ni mwezi wa kumi na moja wa kalenda ya Kiebrania. Ni wakati wa mwisho wa Januari na mwanzo wa Februari kwa kalenda za Kimagharibi.

mwezi wa kumi na mbili

Huu ni mwezi wa kumi na mbili wa kalenda ya Kiebrania. Ni wakati wa mwisho wa Februari na mwanzo wa Machi kwa kalenda za Kimagharibi.

1 Chronicles 27:16

Eliezeri ... Mikaeli

Haya ni majina ya wanaume.

1 Chronicles 27:19

Ishmaia ... Yerohamu

Haya ni majina ya wanaume.

1 Chronicles 27:23

wenye umri wa miaka ishirini au chini zaidi

"watu wenye miaka 20 au chini"

kuongeza Israeli

"kuongeza idadi ya Israeli"

kama nyota za mbinguni

Namba ya watu wa Israeli inalinganishwa na namba ya nyota kuonyesha zilivyo nyingi.

Gadhabu iliangukia Israeli

"Mungu aliwaadhibu watu wa Israeli"

Hii idadi haikuandikwa

"Hakuna aliye andika hii namba chini"

1 Chronicles 27:25

Azimavethi ... Zabdi

Haya ni majina ya wanaume.

mhusika wa

"wajibika kulinda"

minara iliyo imarishwa

"nguzo imara"

walio lima ardhi

Hii ina maana ya kuchimba au kutufua udogo kabla ya kupanda

Shefamu

Hili ni jina la sehemu.

1 Chronicles 27:28

mikuyu

Huu ni aina ya mti

Baali Hanani ... Shitrai ... Adlai

Haya ni majina ya wanaume.

Gederi .. Shafati

Haya ni majina ya sehemu

iliyo kuwa inalishwa

"walio kula nyasi shambani"

1 Chronicles 27:30

Obili ... Yedeia ... Yazizi

Haya ni majina ya wanaume

Mishimaeli ... Mhagri

Haya ni majina ya makabila au koo.

Meronothi

Hili ni jina la sehemu.

Hawa wote

"Hawa wanaume"

1 Chronicles 27:32

Yonathani ... Yehoiada

Haya ni majina ya wanaume.

Waariki

Hili ni jina la kabila la ukoo.

1 Chronicles 28

1 Chronicles 28:1

maafisa

Ona jinsi ulivyotafsiri hii 24:4

kazi walizo pangiwa

Kazi inayohitaji kurudiwa, kwa mfano kila siku au kila mwezi.

wa maelfu na mamia

"1,000s na wa 100s"

mali

Hili neno moja linamaana ya vitu na ardhi mfalme alivyomiliki.

1 Chronicles 28:2

akainuka kwa miguu yake

"alisimama juu"

kaka yangu na watu wangu

Mistari hii miwili inashiriki maana moja na kuweka mkazo kuwa Daudi na watu wa Israeli ni ndugu.

sanduku la agano la Yahweh;stuli ya miguu kwa ajili ya Mungu wetu

Mstari wa pili unaelezea mstari wa kwanza. Yahweh mara nyingi inaelezea "sanduku la agano" kama "stuli yake ya miguu."

hekalu kwa jina langu

"hekalu kwa ajili yangu"

mwanaume wa vita na umemwaga damu

Maelezo yote yanahamasisha kitu kimoja , kwamba Daudi aliuwa watu.

umemwaga damu

"aliuwa watu"

1 Chronicles 28:4

Taarifa za jumla:

Daudi anaendelea kuongea na Waisraeli.

mfalme wa Israeli milele

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi na uzao wake utatawala milele au 2)Daudi ataendelea kuwa mfalme wa Israeli baada ya kufufuka kutoka wafu.

Israeli yote

"ardhi yote ya Israeli'' au "Waisraeli wote"

kuketi katika kiti cha enzi

"kutawala" au "kuwa mfalme wa"

ufalme wa Yahweh, juu ya Israeli

"Israeli ambayo ni ufalme wa Yahweh"

1 Chronicles 28:6

Taarifa za jumla:

Daudi anaendelea kuongea na Waisraeli.

Aliniambia

"Mungu aliniambia"

nyumba yangu

Neno "nyumba" linamaana ya hekalu la Yahweh.

Nimemchagua yeye kuwa mwana wangu, nami nitakuwa baba yake

Hii haimaanishi kwamba Solomoni amekuwa kabisa mwana wa Mungu, ila inaeleza mahusiano binafsi kati yake na Mungu watakayo kuwanayo. "Nimemchagua yeye kumtendea kama mwanangu, na nitakuwa kama baba kwake"

amri zangu na sheria

Haya maneno mawili kwa ujumla yana maana moja inayoelezea kila kitu ambacho Yahweh alikiamuru.

kama ulivyo siku ya leo

Neno "ulivyo" hapa linamuelezea Daudi. "kama ulivyokabidhiwa hii siku"

1 Chronicles 28:8

Taarifa za jumla:

Daudi anaendelea kuongea na Waisraeli.

Kisha sasa

Hii ina ashiria kwamba Daudi ameanza awamu mpya katika hotuba yake.

mshike na kufanya

Maneno haya "kufanya" yanamaanisha kitu kimoja na "mshike" Kwapamoja maneno yanahamasisha umuhimu wa kufanya kile Mungu alicho amuru.

watoto wenu baada yenu

" watoto wenu ambao watachukua nafasi zenu baada ya kufa"

1 Chronicles 28:9

Mungu wa baba yako

Daudi anajiita "baba yako" kwasababu hiii ni tafrija maalumu. "Mungu wangu"

moyo wako wote

"kabisa"

anachunguza mioyo yote na kufahamu amasa ya kila wazo la mtu

Hii mistari miwili ina maana moja na kuweka mkazo kwamba Yahweh anajua mawazo na nia za kila mtu.

Ukimtafuta, ataonekana kwako

"ukijaribu kumpata Yahweh akusikilize wewe, atafanya hivyo"

Elewa

"Ona sasa" "Kumbuka" aua "Kuwa na tahadhari"

Kuwa imara na ufanye

Neno "imara" hapa la husu nguvu ya nia na uweza wa tabia.

1 Chronicles 28:11

baraza la hekalu

"baraza ya hekalu" au "mwingilio wa hekalu" hii ina eleza nguzo zilizo saidia dari katika mwingilio wa hekalu.

hazina

vyumba vya hifadhi vya vitu vya thamani

1 Chronicles 28:13

masharti

Haya yalikuwa maagizo maalumu kuhusu jinsi makuhani na Walawi wafanye kazi katika hekalu.

viitengo

Hii ya husu makundi ambayo makuhani na wafanya kazi wengine wa hekalu walikuwa wamepangwa kufanya kazi zao. Ona jinsi ulivyo tafsiri hili neno 24:1

1 Chronicles 28:18

dhahabu ya kutakasika

"dhahabu iliyo safishwa" au "dhahabu yenye thamani"

Nimeeka haya katika maandishi

"Nimeandika yote haya chini"

kunipa kuelewa

"alinisaidia kuelewa maelekezo"

1 Chronicles 28:20

hodari na mjasiri

Haya maneno mawili yanamanisha kitu kimoja na kukazia kuwa Sulemani lazima awe shujaa.

Usiogope au kuwa na wasiwasi

Haya maneno mawili yanamanisha kitu kimoja na kukazia kuwa Sulemani lazima asikate tamaa. "Kuwa hodari" au "Kuwa Mjasiri"

yupo nawe

"nitakusaidia wewe"

Hatakuacha wala kukutelekeza

Haya maneno mawili yanamanisha kitu kimoja na kukazia kuwa Yahweh ata kuwa daima na Sulemani. "Ata kuwa nawe daima"

hivi ni vitengo vya makuhani na Walawi

Ona jinsi ulivyo tafsiri 28:13

1 Chronicles 29

1 Chronicles 29:1

mawe ya shohamu

Haya ni mawe yenye mistari meupe na meusi yanayo tengenezewa mikufu.

kupangwa

Hii ina maana ya mifumo mizuri ya urembo iliyo undwa na mawe.

1 Chronicles 29:3

Maelezo ya Jumla

Daudi anaendelea kuongea na watu kuhusu vitu anavyo toa kwa ajili ya hekalu.

talanta elfu tatu

"talanta 3,000"

dhahabu kutoka Ofiri

dhahabu bora na ya gharama

1 Chronicles 29:8

hazina

Hii ni sehemu ambayo pesa na vitu vya thamani vimeekwa.

Yehieli

Hili ni jina la mwanaume.

Gerishoni

Huyu alikuwa mzaliwa wa kwanza wa Lawi.

moyo wao wote

kwa utayari, na bila shaka au wasi wasi

1 Chronicles 29:10

Na uabudiwe, Yahweh, Mungu wa Israeli babu wetu, milele na milele

"Na usifiwe, Yahweh baba yetu, Mungu wa Israeli, milele na milele"

1 Chronicles 29:12

Maelezo ya Jumla

Daudi anaendeleza maombi yake sifa kwa Yahweh

Mkononi mwako kuna nguvu na uwezo

Maneno "nguvu na "uwezo" yana maana moja na yanasisitiza ukuu wa nguvu za Yahweh.

1 Chronicles 29:14

Maelezo ya Jumla

Daudi anaendeleza maombi yake sifa kwa Yahweh

Lakini mimi ni nani, na watu wangu ni nani, tustahili kutoa kwa hiari hivi vitu?

Daudi anamaanisha yeye na watu wake hawastahili sifa kwa kumpa chochote Yahweh.

sisi ni wageni na wasafiri mbele zako

"Unajua sisi si wa muhimu"

Siku zetu katika dunia ni kama kivuli

Vivuli vinatokeza na kutoeka haraka.

1 Chronicles 29:16

kwa unyofu wa moyo wangu

"kwasababu ninataka kuwa mkweli na mwaminifu kwa kila kitu ninachofanya"

1 Chronicles 29:18

hifadhi hili katika fikra za watu wako

"eka hili kwenye mawazo na fikra za watu wako milele"

1 Chronicles 29:20

kusujudu mbele

kulala chini na kutaza ardhi kama njia ya kuonyesha heshima ya hali ya juu

1 Chronicles 29:22

mbele za Yahweh

Hili kumtukuza Yahweh.

mara ya pili

Mara ya kwanza imeelezwa 23:1

kumpaka mafuta ya mamlaka ya Yahweh kuwa mfalme

"alipakwa mafuta kutawala juu ya Israeli kwa niaba ya Yahweh"

1 Chronicles 29:24

utii

"uaminifu wao"

Yahweh alimheshimu sana Sulemani na kumkirimia nguvu kubwa

Hii mistari miwili inasisitiza kuwa Sulemani alipokea upendeleo maalumu kutoka kwa Yahweh, uliyo mfanya mfalme mkubwa na mwenye nguvu wa Israeli.

1 Chronicles 29:26

Daudi

Daudi alikuwa mfalme wa kwanza na alimpenda Mungu na kumtumikia.

Yese

Yese alikuwa baba wa Mfalme Daudi, na mjukuu wa Ruthi na Boazi.

tawala

Neno "tawala" la maanisha kumiliki kama mfalme juu ya watu wa eneo la nchi au ufalme. Utawala wa mfalme ni kipindi chake cha kwenye madaraka.

Israeli, Waisraeli, taifa la Israeli

Neno "Israeli" ni jina Mungu alilo mpa Yakobo. La maanisha, "anaangaika na Mungu"

mtawala, watawala, tawala

Neno "mtawala" ni jina linalo eleza mtu mwenye mamlaka juu ya watu wengine, kama kiongozi wa nchi, ufalme, au kundi la dini.

Hebroni

Ulikuwa mji eneo la juu, lenye vimilima vya miamba maili ishirini kusini mwa Yerusalemu.

Yerusalemu

Yerusalemu ulikuwa asili mji wa Wakanani zamani badae ukawa mji muhimu wa Israeli. Upo kilomita 34 magharibi mwa Bahari ya Chumvi na kaskazini mwa Bethlehemu. Bado ni mji mkuu wa Israeli.

kifo, kufa, kafa

Haya maneno yanatumika kutaja mauti ya kimwili na kiroho. Kimwili, inaeleza jinsi mwili wa nyama wa mtu unaacha kuishi. Kiroho, inaeleza wenye dhambi wanapo tengwa na Mungu kwasababu ya dhambi.

chema, wema

Neno "wema" lina maana tofauti kulingana na muktadha. Lugha nyingi zitatumia maneno tofauti kutafsiri hizi maana tofauti.

umri

Neno "umri" la husu idadi ya miaka mtu ameishi. Pia ya tumika kumaanisha kipindi cha muda.

maisha, ishi, kuishi, hai

Haya maneno yote yanaeleza kuwa hai kimwili, sio kufa. Yanatumika pia kimafumbo kumaanisha kuwa hai kiroho.

heshima, kuheshimu

Maneno "heshima" na kuheshimu yana maana ya kumpa mtu adhama, kukweza, au muabudu

1 Chronicles 29:29

yameandikwa katika historia ya Samweli nabii, katika historia ya Nathani nabii, na katika historia ya Gadi nabii

Hii ni kazi isiyo kuwepo tena.

Yalio ekwa kwenye kumbukumbu ni matendo

"Mtu mmoja aliandika hapo matendo"

matendo ya utawala wake

"mambo yaliyo tokea wakati Daudi akiwa mfalme"

mambo yalio mdhuru

"Mambo ya mataifa mengine yaliyo hathiri Israeli"

2 Chronicles 1

2 Chronicles 1:1

Aliimarishawa katka utawala wake

"Selemani alitumia nguvu kubwa juu ya Israeli"

Yahwe

Hili ni jina la Mungu alilojifunulia kwa watu wake katika Agano la Kale. Angalia ukurasa wa tafisiri ya Neno Yahwe kuhusu namna ya kutafsri neno hili

Mungu alikuwa pamoja naye

"Mungu alimshika mkono" au "Mungu alimsaidia

2 Chronicles 1:2

Kiriathi Jearimu

Mji mdogo ulioko kama maili moja magharibi mwa Yerusalemu.

Aliandaa hema

"Simamisha hema"

Bezaleli mwana wa Uri mwana wa Huri.

Haya ni majina ya kiume.

2 Chronicles 1:6

Huko kwenye madhabahu ya shaba.

Selemani akaenda Gibeoni ambako kulikuwa na madhabahu kwenye hema ya kukutania.

2 Chronicles 1:8

Itimie

"Kamilishwa" au "kuwekwa katika ukamilifu".

Watu wengi kama mavumbi ya ardhi.

"Watu wasisohesabika".

Ni nani anaweza kuwaamua watu wako, ambaoa ni wengi kwa Idadi?.

"Hakuna awezaye kuwaamua watu wako wote ambao hawahesabiki"

2 Chronicles 1:12

Kutoka mbele ya hema ya kukutania.

"Mbele ya hema".

2 Chronicles 1:14

Katika miji ya magari.

Hii inataja miji ambayo iliyohifadhi magari yake.

akatengeneza fedha na dhahabu kuwa vitu vya kawaida kama mawe katika Yerusalemu.

Fedha na dhahabu kuwa vitu vya kawaida kama mawe.

na mbao za mierezi kuwa kama miti ya mikuyu iliyomo katika nyanda za chini

"mbao adimu na zenye thamani ziagizwazo mbali zikawa zikapatikana kw wingi sana."

2 Chronicles 2

2 Chronicles 2:1

Hiramu

Hiramu ni jina la kiume.

2 Chronicles 2:4

mkate wa uwepo

Hii inataja vipande 12 vya mkate ambavyo viliw ekwa mbele ya madhabahu.

mwezi mpya

Hiki kilikuwa ni kipindi cha sikuku zilizofanyika kwa kuzingatia hatua maalumu za mzunguko wa mwezi.

Mungu ni mkuu

Hii inamtaja Mungu kuwa muhimu zaidi, siyo kwamba ana umbo kubwa kuliko miungu mingine .

2 Chronicles 2:6

ni nani anayeweza kumjengea Mungu nyumba, kama dunia yote na hata mbigu yenyewe haviwezi kumtosha?

"hakuna anayeweza kumjengea Mungu nyumba kwa sababu hakuna kitu cha ambo anaweza kuenea. Mimi hakuna wa kunilinganisha naye! Ni mtu anayeweza kumtolea dhabihu pekee.

2 Chronicles 2:8

Miti ya msandali.

Hii ilikuwa aina ya mti uliopendwa kwa kutengenezea vyombo vya muziki au michoro.

Kori

Hiki ni kipimo cha ujazo cha zamani (kori moja ni sawa na lita 220 za ujazo)

Ngano ya ardhini

Haya ni maua ya ngano.

Bathi.

Hiki pia ni kipimo cha ujazo cha zamani (Bathi moja ni sawa na lita 22 za ujazo),

2 Chronicles 2:11

Mwenye karama aya busara na uelewa.

Aliyepewa karama ya utambuzi

2 Chronicles 2:13

Hiramu.

Hili ni jina la kiume.

2 Chronicles 3

2 Chronicles 3:1

Mlima Moria.

Hii ni sehemsu ampako alimtoa sadaka mwanaye, Isaka, kwa Mungu.

Arauna Myebusi.

(Tazama: tafsri ya majina)

Siku ya pili ya mwezi wa pili.

Huu ni mwezi wa pili wa kataika Kiebrania. Siku ya pili ni karibu na katikati ya Aprili katika kalenda za Magaharibi. (Tazama: tafisri ya miezi ya Kiebrania na tafsri ya tarehe).

Katika mwaka wa nne.

(Tazama: tafsri ya tarehe)

Sitini...ishirini

"60...20" (Tazama: tafsri ya namba)

Mikono

Mikono ni sawa na urefu wa sentimeta 46.(Tazma: tafsri ya umbali).

2 Chronicles 3:4

Ukumbi

varanda

Mikono.

(Tazama: tafsiri ya umbali)

Akalitengeneza.

"Alifanya"

Ukumbi mkubwa.

Hii ni rejea ya chumba kikubwa, siyo lango.

2 Chronicles 3:6

Vito vya thamani.

Vito ambavyo vilikuwa vizuri, vyenye thamani kubwa, na vitumika kwa ajili ya kupambia.

Parvaimu.

Istilahi ya jumla kwa ajili ya neno mashariki. (Tazama: tafsiri ya majina).

2 Chronicles 3:8

Mikono.

(Tazama:tafsri ya umbali).

Talanta.

(Tazama: tafsiri ya fedha)

Shekeli.

(Tazama: tafsiri ya fedha).

2 Chronicles 3:10

Sanamau mbili za makerubi

Baadhi hutafsiri kifungu kiki kwa kumaanisha kwamba sanamu za makerubi ilikuwa imetengenezwa kwa chuma.

2 Chronicles 3:13

Kitani safi.

"nguo yaenye ubora wa hali ya juu" au "nguo nzuri".

2 Chronicles 4

2 Chronicles 4:1

Mikono.

(Tanzama: tafsiri ya umbali)

Bahari ya mduara ya chuma cha kuyeyushwa.

Hili ni tanki kubwa sana la chuma

Kingo.

Hii ni ncha ya juu ya Kontena.

Mzunguko.

Huu ni umbali kuzunguka sehemu za nje za mduara.

Kumi kutoka ukingo hadi ukingo

"kumi kwa kila mkono".

2 Chronicles 4:4

Robo ya sehemu zao za nyuma.

Hii ni robo ya sehemu ya nyuma ya mnyama mwenye miguu minne. Tazama nene hilo hilo limetumika (pekee katika rejea nyingine katika Agano la Kale, tazama: 7:25).

Mkono.

.(Tazama: tafsiri ya umbali).

Ukingo wake ulikuwa kama ukingo wa kikombe, kama ua la yungi.

Ukingo ulikuwa na ncha laini"(Tazama: tini ta tashibiha)

Mabafu

(Tazama: tafsiri ya ujazo).

2 Chronicles 4:7

Birika.

Hili ni bakuli lenye kina kifupi lililotumia kwa ajaili ya kufulia.

2 Chronicles 4:11

Huramu.

Hili ni jina la kiume.

Mabakuli ya kunyunyizia.

Mabakuli yaliyotumika kunyunyizia madhabahu katika nyumba ya Mungu.

Taji mfano wa upinde.

Kama taji-Sehemu ya juu ya nguzo inaitwa taji:"mabakuli ya juu" au "bakuli la la sehemu za juu."

Nyavu za mapambo.

Hii inataja micjuu katika sehemu za juu za nguzo.horo ya mapambo au muundo wa

2 Chronicles 4:14

Mabirika.

"Mabakuli".

Bahari mpoja.

Hili ni kontena kubwa la kuogea lililopambwa.

Vyombo vingine.

Vifaa vingine au vitu vilivyotumika madhabahuni

Shaba iliyong'arishwa.

Shaba aambayo wafanyakazi waliing'arisha ili iweze kuakisi mwanga.

2 Chronicles 4:17

Sereda.

Hili jina la mji.

Hivyo ndivyo Selemani alivyovitengeneza vyombo hivi vyote.

Selemani hakutengeneza yeye mwenyewe vile vyombo, bali aliamuru vitengenezwe.

Uzito wa shaba haukuweza kujulikana.

"Uzito wa shaba ulikuwa mwingi sana."

2 Chronicles 4:19

Selemani akazitengeza.

Watumishi wa Selemani walitengeneza vitu chini ya amri yake.

Samani zote.

Mabakuli yote na vifaa vyote ambavyo vilitumika katika nyumba ya Mungu.

Mkate wa uwepo.

Angalia jinsi ulivvyotafsiri hili neno katika 2:4.

2 Chronicles 5

2 Chronicles 5:1

Hazina.

Hili ni eneo ambapo vitu hutunzwa au kuhifadhiwa.

2 Chronicles 5:2

Katika sikukuu, aambayo ilikuwa katika wa saba.

Hii ni sikukuu ya makazi ambayo iko katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba katika kalenda ya Kiebrania. Hiki ni kipindi cha Oktoba katika kalenda ya Magharibi.

2 Chronicles 5:4

Vyombo.

Angalia ulivyo tafsiri katika 4:19

Kondoo na maksaai ambao hawakuweza kuhesabika.

"Kondoo na maksai wengi."

2 Chronicles 5:7

Mahali pake.

"Kwenye sehemu yake iliyopangwa"

2 Chronicles 5:9

Hadi leo.

Hii inarejea wakati ampapo kitabu cha 2 Mambo ya Nyakati kiliandikwa.

2 Chronicles 5:11

Asafu, Hemani, Yeduthuni.

Watatu hao hao waliongoza ibada wakati Daudi alipolileta sanduku la agano Yerusalem. Baadaye Daudi aliwachagua kuwa wanamziki wa hekalu. (Tazama: tafsiri ya majina).

Wana na ndugu.

"ndugu zao" au "uzao wao".

Matoazi.

Sahani mbili nyembamba za chuma, ambazo hupigwa pamoja ili kufanya mlio mkubwa (Tazama: tafsiri ya maneno yasiyojulikana).

2 Chronicles 6

2 Chronicles 6:1

Makao makuu.

"Sehemu ya kuishsi ya heshima sana."

Kusanyiko lote la Israeli walaikuwa wamesimama.

"Watu wakiwa wamesimama."

2 Chronicles 6:4

Ili jina langu liwe humo.

"Ili kujifanya mwenyewe nijulikane huko".

Ametimiza kwa mkono wake mwenyewe.

Amewezesha kutokea au amehakikisha kwamba ahadi hizi zinatimia.

2 Chronicles 6:7

Ndani ya moyo wa Daudi.

"Nia ya Daudi."

Kwa ajili ya jina la Yahwe

Jina la Yahwe linawakilisha uwepo wake kamili.

2 Chronicles 6:10

Ambamo kuna agano la Yahwe.

"Ambamo kuna meza za za mawe zikionesha aganao alilofanya Yahwe nasi watu wa Israeli. "

2 Chronicles 6:12

Mbele ya kusanyiko lote la Israeli.

"Mbele ya watu wa Israeli ambao walikuwa wamekusanyika huko."

Mikono.

Kipimo cha zamani.

Akanyosha mikono yake kuzielekea mbingu.

Selemani alinyosha mikono yake na kuilekeza juu huku akipiga magoti juu ya jukwaa ili aombe.

2 Chronicles 6:14

Watumishi wako ambao hutembea mbele zako kwa moyo wako wote.

"Sisi ambao hujibidisha kikamilifu kufanya kile unachotutaka tufanye".

Ulisema kwa kinywa chako na umetimiza kwa mkono wako.

Hii ina maanisha ahadi ambayo Mungu alifanya na Daudi kwamba mwanaye atamjengea hekalu: "Umetimiza ahadi ahadi yako."

2 Chronicles 6:16

Tunza.

Hili ni ombi: "tafadhali fanya"

Hautashindwa kupata mtu mbele yangu wa kukaa juu ya kiti cha enzi cha Israeli.

"Siku zote utakuwa na mfalme kutoka miongoni mwa uzao wa Daudi."

Kama ulivyotembea mbele zangu.

"Katika namna ambayo Daudi alifanya."

2 Chronicles 6:18

Lakini kweli Mungu ataishi na wanadamu juu ya dunia?.

"Lakini Mungu, kwa hakika hutaishi kabisa na wanadamu juu ya dunia." (Tazama: tini rg rquestion).

dunia yoye na mbingu yenyewe.

Angalia ulivyoitafisiri hii katika 2:6.

Sikia kilio na maombi.

Neno "kilio" na "maombi" yana maana moja. Kwa pamoja yanaweka msisitizo wa maombi yake: nakusihi jibu maombi yangu ya kumaanisha." (Tazama: tini double)

Ambapo uliahidi kuliweka jina lako.

"Ambapo ulisema utawafanya watu wakujue".

Fumbua macho yako kuelekea hekalu hili usiku na mchana.

Tafadhali wasaidie wanaokuja kwako katika "hekalu, wakati wowote—usiku au mchana."

Maombi atakayaoomba mtumishi wako kuelekea sehemu hii.

Mwandishi anaomba akiwa ameelekea Hekalu.

2 Chronicles 6:21

Un anaposiki, samehe.

"Unaposikia maombi, tafadhali wasamehe dhambi zao."

2 Chronicles 6:22

Ili kuyaleta matendo yake juu ya kichwa.

"Kwa kumwadhibu kama anavyostahili kuadhibiwa" (Tazama: tini ....)

2 Chronicles 6:24

Bsi tafadhali sikia mbinguni na usamehe zao

"Tafadhali, yaheshimu maombi yao" Tazma: tini .....)

2 Chronicles 6:26

Wakati mbingu zimefungwa na hakuna mvua

Kirai, "mbingu zimefungwa" kina maana kwamba hakuna mvua inayoshuka kutoka mawinguni. "Wakati utakapoacha kuruhusu mvua yoyote kunyesha." (Tazama: tini ..........)

Wakilikili jina lako.

Kwa maneno yao na matendo yao, wanamweshimu Mungu na mamlaka Yake. (Tazama: tini ......)

Kuziacha dhambi zao.

Kuziacha njia zao mbaya".

Utakapowaelekeza kwenye njia njema iwapasayo kutembea

"Kuwaonesha jins ya kuishi kwa haki".

2 Chronicles 6:28

Kila mmoja akilijua pigo na huzuni katika moyo wake.

Maana yake yaweza kuwa: "akijua dhambi katika moyo wake" au "akijua moyoni mwake kwamba mapigo na hudhuni ni matokeo ya dhambi zake mwenyewe".

Akinyosha mikono yake.

Angalia tafsir ya mstari wa 2:12.

Njia zake zote.

"Alichofanya".

2 Chronicles 6:32

Ukuu wa jina lako, mkono wako wenye nguvu, na mkono wako ulionyoshwa.

"Wewe ni mkuu sana na mwenye nguvu sana". (Tazama: tini ......)

Inaitwa kwa jina lako.

Inayojulikana kama nyumba ya Yahwe, mali yako"

2 Chronicles 6:34

Nimeijenga.

"Watu wamejenga chini ya uongozi wangu" Tazama: tini synecdoche)

2 Chronicles 6:36

Taarifa za jumla:

Tazama: tini mfano.

Adui wakawabeba na kuwachukua kama mateka kwa ajili ya nchi zao.

Adui wakiwachukua mateka na kuwapeleka kwenye nchi ya adui zao.

Kuomba kukabili nchi yao.

Hii inarea Israeli. "Na ikiwa wataomba kukabili nchi yao uliyowapa babu zao"

2 Chronicles 7

2 Chronicles 7:1

Kwa nyuso zao juu ya sakafu.

Huu ni mkao wa maombi. "Walisudu kwa nyuso zao zikigusa sakafu ya mawe.

Agano lake la kifalme.

"Uaminifu wa agano la Mungu" au Mungu ameahidi kuwapenda milele watu wa Israeli."

2 Chronicles 7:4

Kila mmoja akasimama mahali pake pa kuhudumu.

"Kila mmoja akasimama mahali pake alipopangiwa".

2 Chronicles 7:7

Haikuweza kuzibeba sadaka za kuteketezwa.

"Haikuweza kubeba kiasi kingi cha sadaka za kuteketezwa"

2 Chronicles 7:8

Na Israeli wote pamoja naye,

Watu walikuja kutoka Israeli yote.

Lebo Hamathi

Lebo Hamathi ni jina na mahali

Kusanyiko la makini

Hili lilikuwa kusanyiko maalumu la kidini.

Katika siku ya ishini na tatu ya mwezi wa saba.

Siku ya tatu ya mwezi wa saba - Hii ni siku ya mwezi wa saba wa kalenda ya Kiebrania. Siku ya ishirini na tatu ni karibu na katikati ya mwezi wa Oktoba. Katika Kalenda za magharibi.

Kwa furaha na mioyo ya shangwe.

Neno "furaha" na "shangwe" yana maana ya akitu kimoja. Kwa pamoja yanasistiza nia ya furaha (kwa mioyo ya furaha sana)

2 Chronicles 7:11

Alikitimiza kwa.

"Alikikamilisha"

Nimesikia maombi yako.

"Nimeyasikiliza maombi yako".

2 Chronicles 7:13

Kama nitazifunga mbingu ili kwamba kusiwepo mvua.

"Kuizuia mvua" (Tazama: Mifano).

Waimeze nchi.

Neno "nchi" limetumika kumaanisha ",mimea na mazao yote"

Kuutafuta uso wangu.

"Kumtafuta Mungu" au kujaribu kumfanya Mungu akupe usikivu".

Macho yangu yatakuwa wazi na masikio yangu yatasikiliza.

Maneno "macho" na "masikio" yana maana ya Mungu, ambaye huchagua kuona na kusikia maombi yao: "Nitawaona na nitawasikiliza"

2 Chronicles 7:16

Mach yangu na moyo wangu.

"Upenddo wangu. kutazama kwa makini, na kulinda.

Kama utatembe mbele zangu kama baba yako Daudi alivyotembea.

"Kama utanitii kama Baudi, baba yako alivyofanya."

Nitakithibitisha kiti cha enzi cha enzi.

"Nitahakikisha kwamba uzao wako siku zote watakuwa wafalme," (UDB).

2 Chronicles 7:19

Nitawang'oa kutoka kwenye nchi yangu amabayo nimewapa.

"Nitawaondoa kwenye nchi yangu." Inafanalinganisha kuvuta mizizi ya mimea kwa kuindoa kwenye ardhi, na kuondolewa kwa watu wa Mungu kutoka kwenye nchi yake. Matokeo yake yatakuwa kuangamia kwa na huzuni ya watu.

2 Chronicles 8

2 Chronicles 8:1

Ikawa karibu ya mwisho wa miaka ishirini.

Baada ya miaka 20.

Hiramu.

Hili ni jina la kiume.

2 Chronicles 8:3

Selemani akauvamia Hamathzoba.

Selemani anawakilisha jesji lake la vita lote. "Jeshi la Selemani likauvamia mji wa Hamathzoba".

Tadmori...Hamathi.

Miji iliyoko Siria.

2 Chronicles 8:5

Taarifa za jumla.

Tazama tafsiri ya majina

2 Chronicles 8:7

Ambao waliachwa baada yao katika nchi

"Ambao walisalia katika nchi"

Akawafanyisha kazi kwa nguvu.

Akawafanya watumwa.

Hata leo.

Hii inataja wakati ambapo kitabu cha 2 Nyakati kilipoandikwa.

2 Chronicles 8:9

250

Mia mbili hamsini(250).

2 Chronicles 8:12

Ukumbi.

Huu ni ukumbi uliofunikwa au njia ya kuingilia ulioshikiliwa na nguzo kwenye jengo.

Kwa kufuata maelekezo yaliyokuwa katika amri

Kwa mujibu wa maagizo ya ya sheria ya Musa.

2 Chronicles 8:14

Watu hawa hawakupotea kutoka kwenye amri.

Watu walizifuata amari.

2 Chronicles 9

2 Chronicles 9:3

Ikulu aliyokuwa amejenga, 4chakula mezani kwake, mahali pa kukaa watumishi wake, kazi ya watumisshi wake na mavazi yao.

Beth Sheba aliona mambo yote ya Selemani ya kushangaza.

Wabeba kikombe.

Hawa walikuwa watumishi walio onja kinywaji kabla mfalme hajanywa ili kupima kama haina sumu.

Hapakuwa na roho zaidi ndani yake

"Hakujaa akiburi tena".

2 Chronicles 9:5

Na sasa macho yangu yamekiona.

"Sasa nimejionea mimi mwenyewe".

Sikuambiwa nusu ya kuhusu hekima na utajiri wako.

"Wewe una hekima na ni tajiri kupita kawaida"

2 Chronicles 9:7

Ambao husimama mbele yako.

"Ambao husubiri amfri zako mbele zako"

Ambaye amepata raha ndani yako.

"Ambaye amependezwa nawe"

2 Chronicles 9:9

Talanta.

Aina ya fedha iliyotumika katika ssiku za Agano Jipya

2 Chronicles 9:10

Hiramu.

Mfalme wa Tiro

Ofiri.

Sehemu isiyojulikana iliyojulikana kwa dhahabu zake.

Miti ya msandali.

Hii ni aina ya mbao.

2 Chronicles 9:13

666.

Mia sita sitini na sita

2 Chronicles 9:15

Shekeli mia sita za dhahabu zilitumika kwa kila ngao.

"Zilitengenezwa kwa shekeli mia sita za dhahabu".

Shekeli...minas

Shekeli na mina ni mojawapo ya vipimo ambavyo watu wa zamani hasa nyakati za Agano la Kale walitumia kwa sababu hawakuwa na vipimo vya kisa kama vile kilo, mita nk. Shekeli 1 ilikuwa sawa na graamu 1, na mina au shekeli 50 ilikuwa sawa na kilo 0.57.

Ikulu ya Mstu wa Lebanon.

Hii ilikuwa kama sehemu ya kuhifadhia iliyotengenezwa kwa mbao nyingi kubwa kutoka Lebanoni, ilikuwa karibu na ikulu. Kwa jina jingine iliitwa Amori.

2 Chronicles 9:17

Pembe.

Hii ilikuwa kazi nyingine ya pembe ya mnyama kama tembo au faru.

Na sehemu ya juu ya kiti cha enzi ilikuwa duara

"Sehemu ya juu nyuma ya kiti cha enzi ambapo mfalme aliketi ilikuwa ya duara".

2 Chronicles 9:19

Fedha haikuchuliwa kuwa ya thamani katika siku za Selemani.

Katika siku za Selemani fedha haikuwa kitu cha thamani.

Nyani na tausi.

Wanyama kutoka mbali sana, kama vile Afrika

2 Chronicles 9:22

Ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake.

"Ambayo Mungu alimpa".

Mwaka baada ya Mwaka.

Kila mwaka

2 Chronicles 9:25

Taarifa za jumla:

Selemani aalikuwa na mazizi elfu nne (4,000), na wapanda farasi kumi na mbi elfu (12,000)

Mazizi.

Hii ni boma ndogo ambamo farasi huhifadhiwa

2 Chronicles 9:27

Nyingi kama mawe juu ya ardhi.

Fedha nyingi sana.

Akazifanya mbao za mierezi kuwa nyingi kama mikuyu ambayo iko nyanda za chini.

"Nyingi sana"

Kutoka nchi zote.

"Kutoka nchi zote jirani" au kutoka nchi zote".

2 Chronicles 10

2 Chronicles 10:1

Israeli wote.

"Watu wote wa taifa la Israeli".

Mwana wa Nebati.

Nebati ni jina la kiume.

2 Chronicles 10:8

Rehoboamu akapuuza ushauri.

"Rehoboamu hakufuata ushauri"

Wanaume vijana.

"Wanaume vijana" jinsi wasivyo na hekima na uzoefu katika mambo ukilinganisha na wanaume wazee ambao walikuwa washauri wa Selemani.

Ambao walikuwa wa rika lake, ambao walisimama mbele yake.

Waliokuwa rafiki zake wa muda mrefu, walimshauri.

2 Chronicles 10:10

Kidole changu kidogo ni kinene kuliko kiuno cha baba yangu.

Pointi ya Rehoboamu ni kwamba yeye ni katilina mwenye aamri kuliko baba yake.

Nitawaadhibu kwa ng'e.

"Lakini nitawapiga kwa mijeredi yenye vipande vya chuma."

2 Chronicles 10:12

Watu wote

"Viongozi wote"

Siku ya tatu.

Siku ya tatu.

2 Chronicles 10:15

Ahiya Mshiloni...Yeroboamu mwana wa Nebati.

Ahiya, Nebati na Yeroboamu, haya yote ni majina ya kiume.

2 Chronicles 10:16

Tunasehemu gani katika Daudi?

"Hatutaki kufanya kitu chochote na hawa uzao wa Daudi".

2 Chronicles 11

2 Chronicles 11:1

Wanaume waliochaguliwa ambao walikuwa wanajeshi.

"Wanajeshi wake bora"

2 Chronicles 11:2

Neno la Yahwe ,ikamjia.

"Yahwe alisema neno lake"

Shemaya.

Shemaya ni jina mtu wa jinsia ya kiume.

2 Chronicles 11:5

Maelezo ya jumla.

Hii ni miji ambayo Yeroboamu aliijenga katika Yuda na Benyamini.

2 Chronicles 11:11

Yuda na Benyamini zikawa zake.

Yeroboamu alikuwa mmiliki wa mipaka ya Yuda na Benyamini.

2 Chronicles 11:13

Makuhani na walawi waliokuwa katika Israeli yote wakaenda kwake

"Makuhani na Walawi wakatoka Israeli, ufalme wa Kaskazini ili waende Yuda".

Nchi za malisho

Nchi zilizokuwa kwa ajili ya kuchungia wanyama.

2 Chronicles 11:16

Watu kutoka kabila zote za Israeli wakaja nyuma yao, wale walio wameiilekeza mioyo yao kumtafuta Yahwe.

Watu kutoka makabila ya ufalme wa Kaskazini(Israeli) ambao walikuwa bado wanamwabudu Bwana Mungu walikimbilia Yuda.

Wakatembea kwa miaka mitatu katika njia ya Daudi na Selemani.

"Waliufuata mfano wa Daudi na Selemani kwa miaka mitatu".

2 Chronicles 11:18

Taarifa za jumla:

Mahalathi ni jina la kike.

2 Chronicles 11:20

Maelezo ya jumla:

Mahalathi alikuwa binti wa Yerimothi. Mfalme Rehoboamu alimuoa huyu binti akawa mkewe, baadaye Rehoboamu huyu huyu alimuoa Maaka, yaani binti wa Absalomu.

2 Chronicles 11:22

Taarifa za jumla:

Rehoboamu ni jina la kiume, na huyu ndiye alikuwa mfalme wa yuda. Abiya ni jina la kiume pia.

2 Chronicles 12

2 Chronicles 12:1

Ikawa akwamba

"Ikawa kwamba" ni maneno yanayoashiria tukio muhimu katika historia; yaani wakati ule ule jambo lilipotokea".

Na Israeli wote pamoja naye

"Israeli na Yuda wote walimfuata katika dhambi yake." Israeli hapa inajumuisha Yuda pia.

2 Chronicles 12:2

Akaja kinyume.

"Akaja kuvamia au kupiga"

Askari wasio hesabika

"Wanajeshi wengi sana"

2 Chronicles 12:5

Taarifa za jumla:

Shemaya alikuwa nabii katika yuda wakati wa utawala wa mfalme Rehoboamu.

Kwa hiyo pia nimewaweka katika mkono wa Shishaki.

"Kwa hiyo nimewatia katika mikiono ya Shishaki kama mateka"

2 Chronicles 12:7

Wamejinyenyekeza.

"Mfalme na viongozi wengine wa Israeli walikuwa wamejinyenyeza wenyewe," Mfalme na viongozi wengine ni maneno yanayowakilisha au yenye maana ya watu wote wa Isaraeli.

Neno la Yahwe likamjia.

"Yahwe alisema neno lake."

Nitawaokoa kwa hatua fulani.

Nitawaokoa wasiangamie kwa kabisa kabisa

Hasira yangu haitamiminwa juu ya Yerusalemu.

"Sitaiachilia hasira yangu yote dhidi ya Yerusalemu"

2 Chronicles 12:9

Kuzikabidhi mikononi mwa maamri jeshi

"Kuziweka mikononi mwa maamri jeshi"

2 Chronicles 12:11

Ikawa kwamba Mfalme kila alipoingia.

Inaashiria tukio malumu katika historia. Lugha nyingi zina namna yake ya kusema kipindi hiki muhimu.

Gadhabu ya Yahwe ikampisha mbali, kwa hiyo hakuwaangamiza kabisa kabisa.

"Yahwe hakuwa na hasira naye tena, na kwa hiyo hakumwaangamiza kabisa kabisa"

Pembeni.

"Kwa nyongeza "

2 Chronicles 12:13

Ili kwamba aliweke jina lake humo.

"Ili kwamba aheshimiwe humo siku zote.

Hakuuelekeza moyo wake kumtafuta Yahwe

"Hakuwa na nia na nguvu za kumtii Mungu".

2 Chronicles 13

2 Chronicles 13:1

Maaka, binti wa Urieli wa Gibea.

Maaka alikuwa mama mzazi wa Abiya, mfalme wa Yuda ambaye alipigana vita na Yeroboamu.

2 Chronicles 13:4

Mlima Semaraimu.

Mlima Semaraimu ulikuwa katika mji wa Semaraimu

Hamjui kwamba...agano?

"Mnajua vizuri sana kuhusu agano langu nililofanya na Daudi.

2 Chronicles 13:6

Mwana wa Nebati

Nebati alikuwa baba yake Yeroboamu mfalme wa Israeli.

Washirika wa karibu

"Watu wenye tabia mbaya, wasio na maadili".

Wakamkusanyikia

"Wakaungana pamoja na Yeroboamu".

2 Chronicles 13:8

Ndama wa dhahabu ambao Yeroboamu alitengeneza kama miungu.

Hii ina maana ya miungu aliyotengeneza Yeroboamu.

Hamkuwafukuza...Walawi?

"Mmewafukuza Walawi"

Hamkujifanyia makuhani katika namna ya watu wa nchi zingine.

"Mmejifanyia makuhani kama vile wajifanyiavyo watu wa nch zingine.

Yeyote ajaye kujitakasa mwenyewe na ngo'mbe dume kijana, na madume ya kondoo anaweza kuwa kuhani wa kile ambacho siyo. miungu.

"Yeyote atoaye ng'ombe dume na madume saba ya kondoo anaweza kuwa kuhani wa sanamu tu ambazo hazina hadhi ya kuitwa miungu"

2 Chronicles 13:10

Ambao wako katika kazi zao

"Wanaofanya kazi"

Mkate wa uwepo

"Mkate wa uonyesho" ulikuwa mkate maalum ambao ulitengenezwa kama ishara ya uwepo wa Mungu na ushirika wake na watu wake.

Pia huweka kinara cha dhahabu pamoaja na taa zake

"Pia hukitunza au kukiangalia kinara cha dhahabu"

2 Chronicles 13:12

Msipigane na Yahwe.

Hii ni lugha ya picha inayowataka wahusika hawa wasiende kinyume na mapenzi ya Yahwe (msipigane na Yahwe)

2 Chronicles 13:13

Mavamizi nyuma yao.

Yeroboamu alijipanga na kufanya mavamizi ya kushtukiza nyuma ya jeshi laYuda

Mavamizi yalikuwa nyuma yao.

Mavamizi ya ghafla au kushtukiza yalikuwa nyuma ya jeshi la Yuda.

Wakamlilia Yahwe.

Walimwita Yahwe kwa sauti kubwa sana.

Ikawa kwamba Mungu akampiga.

Mungu alimuacha Yeroboamu akapigwa na adui zake.

2 Chronicles 13:16

500,000

Laki tano(hii ni idadi ya watu waliouawa na Abiya)

2 Chronicles 14

2 Chronicles 14:1

Abiya akalala pamoja na babu zake

"Hii ina maana kwamba Abiya akafa na kuzikwa pamoja na babu zake.

Katika siku zake.

Katika kipindi cha utawala wake.

Katika siku yake nchi ilikuwa tulivu kwa miaka kumi.

"Palikuwa na amani katika nchi kwa miaka kumi"

Katika macho ya Yahwe Mungu wake

"Kama Yahwe atakavyo"

2 Chronicles 14:5

Akaziondosha mbali sehemu za juu na madhabahu za kufukiza kutoka miji yote ya Yuda

Asa aliharibu kila aina ya madhabahu ambayo ilitumika kuabudia miungu ya uongo katika Yuda

2 Chronicles 14:7

Taarifa za jumla:

Wanaume laki tatu (300,000), wanaume laki mbili na themanini elfu (280, 000).

Asa aliwaambia Yuda

Asa aliwaambia watu wa Yuda

Tumemtafuta Yahwe Mungu wetu

Tumemwomba Yahwe Mungu wetu kutusaidia.

2 Chronicles 14:9

Taarifa za jumla:

Zera alikuwa mfalme wa Ethiopia, ambaye alitoka na jeshi la wanajeshi milioni moja (1,000,000), na magari mia tatu (300) kwenda kupigana na mfalme Asa.

Maresha

Maresha ulikuwa mji katika Yuda

Usimuache mtu akushinde

"Enyi watu msiwaruhusu watu wengine kuwashinda"

2 Chronicles 14:12

Waethiopia

Waethiopia walikufa kwa sababu Yahwe aliwaua

2 Chronicles 15

2 Chronicles 15:1

Roho wa Mungu akaja juu ya Azaria

Roho wa Mungu alimpa Azaria uwezo wa kutabiri.

Odedi.

Odedi alikuwa alikuwa mtoto wa kiume wa Azaria.

2 Chronicles 15:3

Isareli hawakuwa na Mungu wa kweli

Israeli walikuwa wameacha kumtii Mungu

.Bila kuhani wa kuwafundisha.

"Hawakuwa na kuhani wa kuwafundisha"

Wakampata

"Mungu aliwaitikia Waisraeli walipomtafuta".

2 Chronicles 15:6

Waligawanyika vikundi, taifa dhidi ya taifa, na mji dhidi ya mji

Walishindwa na mataifa na miji mingine.

2 Chronicles 15:8

Unabii wa Odedi nabii

Matoleo mengi, likiwemo na UDB, yanasomeka, "Unabii wa Azaria, mwana wa Odedi nabii." Yanasomeka hivyo ili kuleta ujumbe unaokubaliana na 15:1. Watafsiri bila shaka watataka kufanya maana hii hii katika matoleo yao.

Kuviondosha mbali vitu vya kuchukiza

"Aliziondoa sanamu"

Yahwe Mungu wake alikuwa pamoja naye

"Yahwe alikuwa akimsaidia".

2 Chronicles 15:10

Kwa hiyo walikusanyika

Hawa ni makabila ya Yuda na Israeli yaliyokuwa pamoja na Asa.

Mwezi wa tatu.

Huu ni mwezi wa tatu wa kalenda ya Kiebrania

Ni mwezi unaotokea mwishoni mwa Mei na mwanzoni mwa Juni kaatika kalenda ya magharibi

Tatu...kumi na tano

Tatu(3)...Kumi na tano (15)

Mwezi wa tatu.

Mia saba...elfu saba

Mia saba (700)...Elfu saba (7,000)

2 Chronicles 15:12

Kwa moyo wao wote na kwa roho yao yote

Wakamtafuta Yahwe na Mungu kwa uaminifu na ukamilifu

Kuuawa.

Kutolewa uhai(kuuawa)

2 Chronicles 15:14

Walimuona

Angalia 2 Mambo ya Nyakati 15:4.

Yuda wote wakakifurahia

"Watu wengi walioishi Yuda walifurahia".

2 Chronicles 15:16

Taarifa za jumla:

Maaka ni jina la kike na Asa ni jina la kiume. Maaka alikuwa malkia, yaani mke wa mfalme Asa.

Sanamu ya kuchukiza

Sanamu

Moyo wa Asa ulijito kikamilifu siku zake zote

Asa alimtii na kumfuata Yahwe maisha yake yote. .

2 Chronicles 16

2 Chronicles 16:1

Akaujenga Rama

Hapa "akaujenga ina maana ya kujenga kuta kuzunguka mji ili kwamba mji uweze kulindwa dhidi ya wavamizi".

2 Chronicles 16:2

Beni Hadadi

Ben Adadi alikuwa mfalme wa Aramu.

Ili kwamba aniache.

"Asinivamie."

2 Chronicles 16:4

Akatuma maakida wa jrshi dhidi ya miji ya Israeli

Akatuma majeshi yake kuivaamia miji

Iyoni, Dani, Abelimaimu...miji ya kuhifadhia ya nafutali

Hii ni miji katika Israeli

Akaisitisha kazi yake

Aliyaamuru majeshi yake kuacha kuuzungushia ngome Rama na kufanya kazi zingine huko"

Mbao.

Mbao ni vipande vikubwa vya miti vitumikavyo kujengea nyumba au kuta.

2 Chronicles 16:7

Hanani

Hanani alikuwa mwonaji wakati wa utawalaa wa mfalme wa Yuda.

Waethiopia na Walubi hawakuwa jesi kubwa, wenye magari mengi na wapanda farasi wengi?

Waethiopia na Walubi walikuwa jeshi kubwa, lenye magari na wapanda farasi wengi sana

2 Chronicles 16:9

Macho ya Yahwe yanaona kila mahali

Yahwe anaona kila kinachotokea katika dunia yote.

ili kwamba ajioneshe mwenyewe shujaa kwa niaba ya wale amabao mioyo yao ni mikamilifu kumwelekea yeye

"Na Yahwe hulinda kwa nguvu zake"

2 Chronicles 16:11

Kutoka mwanzo hadi mwisho.

Kila kitu alichofanya.

Kitabu cha Wafalme wa Yuda na Israeli

Hiki ni kitabu ambacho hakipo tena.

Asa alipata ugonjwa kwenye miguu yake

"Asa alikuwa na ugonjwa kwenye miguu yake"

2 Chronicles 16:13

Asa akalala pamoja na babu zake

Hii ina maana kwamba "Asa alikufa".

Kitanda

Kitanda hiki ni mfano wa meza ambayo juu yake mwili wa marehemu huwekwa juu yake wakati wa mazishi.

Manukato na aina mbali mbali ya dawa zilizotayarishwa na wale mafundi wa manukato

Kuweka mmea ambao hunukia vizuri kwenye mwili wa marehemu ilikuws mojawapo ya taratibu za mazishi kwa watu wa Isareli. "Mimea ya manukato ya kunukia yalitengenezwa na mtu aliyekuwa na ujuzi katika mambo ya utamaduni.

2 Chronicles 17

2 Chronicles 17:1

Akajiimarisha dhidi ya Israeli

Wazo la "kujiimarisha mwenyewe" jeshi la mfalme. Alilitayarisha jeshi likawa tayari kwa ajili ya kupigana vita na Israeli.

Magereza.

Hizi ni kambi za jeshi kwa ajili ya ulinzi.

2 Chronicles 17:3

Alitembea katika njia ya baba yake.

Tabia inazungumzwa kama kutembea. "Aliishi katika njia za haki kama babu zake waliomtangulia.

Hakuwatafuta mabaali.

Hakuiabudu miung ya Baali ili kutafuta msaada kwayo

2 Chronicles 17:5

Maashera.

Reejea sura ya 14:1

2 Chronicles 17:7

Katika mwaka wa tatu

Ulipofika mwaka mwaka wa 3

Ben-haili, Obadia, Zekaria, Nethania, na Mikaya...Shemiramothi, Yehonathani, Adoniya, Tobia, na Tob-adonia, Elishama na Yehoramu

Haya yote ni majina ya kiume

2 Chronicles 17:10

Hofu ya Yahwe ikashuka juu ya falme zote za nchi.

"Watu katika falme zote za karibu na Yuda wakaogopa sana kwa sababu ya kile ambacho Yahwe angeweza kufanya ili kuwaadhibu.

2 Chronicles 17:14

Adna...Yehonani...Amasia mwana wa Zikri.

Haya ni majina ya majemedari maarufu walikuwa wakiongoza vikosi vya jeshi katika Yuda.

300,000...280,000...200,000

Laki tatu(300,000), Laki mbili na themanini elfu (280,000), Laki mbili (200,000)

2 Chronicles 18

2 Chronicles 18:1

Alifanya undugu na Ahabu.

"Alifanya undugu na Ahabu" au alijifanya mwenyewe kuw rafiki wa Ahabu".

Mimi ni kama wewe, na watu wangu ni kama watu wako.

Yehoshafati anaelezea kuhusu mapatano yake na Ahabu; "Najitoa mwenyewe na wanajeshi wangu kwako ututumie upendavyo."

2 Chronicles 18:6

Hakuna nabii mwingine...ushauri

"Nina uhakika kwambaatakuwepo hapa...ushauri".

Mikaya mwana wa Imla.

Alikuwa nabii wa Bwana.

2 Chronicles 18:9

Mwana wa Kenaani.

Zedekia aalikuwa mmoja wa manabii wa uongo.

Pembe za chuma.

Hii inamaana ya pembe za ng'ombe (kambaku) lakini zilizotengenezwa kwa chuma.

Mtawasukuma Waaramu hadi waangamie."

"Mtawashinda".

Yahwe ameutia kwenye mkono wa mfalme.

"Yahwe atawapa ushindi"

2 Chronicles 18:12

Mikaya

Angalia sura ya 17:7.

Tafadhali maneno yako yawe kama mmoja wa wao na sema mambo mema.

Hii ni rejea kwa maneno yote ya ujumbe wa manabii.

Kwa kinywa kimoja.

"Kwa wazo moja" au "kwa kukubaliana wote".

Kama Yahwe aishivyo.

"Nawahakikishia kuwa jambo hili ni kweli."

Au la?

"Au hatupaswi kuenda".

2 Chronicles 18:15

Ni mara angapi ninapaswa kukutaka akuapa kutoniambia kitu chochote ispokuwa kweli katika jina la Yahwe?

"Nilishakwambia kwamba unapaswa kusema au kuniambia ukweli tu katika jina la Yahwe"

Kama kondoo wasio na mchungaji.

"Wasio na uongozi mzuri"

2 Chronicles 18:17

Sikukuumbia kwamba asingeweza kutabiri mema juu yangu, bali majanga tu?

"Nilikwambia kwamba lazima angetabia kwamba majanga yatanipata".

2 Chronicles 18:19

Kumrubuni.

Hii ina maana ya kumvutia mtu kwa kumpa kitu cha kuvutia.

Kuanguka.

"Kuumia sana " au "kufa"

Mmoja alaisema hivi na mwingine hivi.

Hii inaashiria kwamba palaikuwa na maoni au mawazo zaidi ya moja.

2 Chronicles 18:20

Roho ya uongo katika vinywa vya manabii wake wote.

"Roho inayowafanya manabii kudanya".

2 Chronicles 18:22

Ametanagaza aamajanga kwa ajili yako.

"Amethibitisha kwamba wambo ya ajibu yatakupata."

2 Chronicles 18:23

Zedekia mwana wa Kanaani

Huyu siyo Zedikia aliyetajwa ahapo juu, bali ni nabii mwaminifu kwa Ahabu.

Kwa anjia gani Roho wa Yahwe alitoka kwangu ili aseme nawe?

"Roho wa Mungu hakutoka kwangu ili aje kusema nawe."

Mtakapokimbia katika baadhi ya vyumba vya ndani kwa ajili ya kujificha.

"Mtakapokimbia, kwa hofu kujificha."

2 Chronicles 18:25

Mfalme wa Israeli.

Anayetajwa ahapa ni Ahabu

Amoni.

Hili ni jina la kiume.

Kama utarudi salama, Yahwe hajasema nami.

Mikaya amajua na ana hakika kwamba Yahwe kasema naye.

2 Chronicles 18:28

Wakaenda juu.

"Walipigana dhidi"

Ramothi-giledi.

Angalia sura ya 18:1.

Nitajibadilisha

Hii ina maana ya kujibadilisha mwonekano wa kila siku kwa lengo la kutotambuliwa.

Msiwavamie wanajeshsi wasio wa muhimu wala wanajeshi muhimu.

"Msivamie yeyote miongoni mwa wanajeshi hao"

2 Chronicles 18:31

Yule ni mfalme wa Israeli.

Yehoshafati kwa bahati mbaya walimfananishwa na mfalme wa Israeli kwa sababu Ahabu alikuwa amesistiza kwamba mfalme huyo anakawaida ya kuvaa kifalme.

Mungu akawageuza nyuma kutoka kwake.

"Mungu aliwasababisha wasiendelee kumwelekea"

2 Chronicles 18:33

Kati kati ya maungio ya mavazi yake.

Hii ni sehemu ampapo vipande viwili vya maungi hukutana na huandamwa na mishale na upanga wakati wa vita.

2 Chronicles 19

2 Chronicles 19:1

Mwana wa Hanani.

Yuhu ni jina la mwanaume alikuwa mtoto wa Hanani.

Unapaswa kuwa unawasaidia waovu? Unapaswa kuwapenda wanaomchukia Yahwe?

"Hupaswi kuwasaidia waovu! Hupaswi kuwapenda wale wamchukia Yahwe"

Maashera.

Angalia sura ya 14:1

Umeukaza moyo wako.

"Kuamua kwa nguvu au kikamilifu"

2 Chronicles 19:4

Akawarudisha akwa Yahwe.

"Akairejesha imani yao kwa Yahwe"

2 Chronicles 19:6

Iache hofu ya Yahwe iwe juu yanu.

"Unapohukumu unapaswa kumkumbuka Yahwe"

2 Chronicles 19:8

Nyumba za mababu wa Israeli.

Familia za mababu wa Israeli.

Kwa ajili ya kufanya hukumu.

"Kusaidia kutatua mabishano"

Kwa moyo wako wote.

Kufanya jambo kwa kujitoa au kwa bidii.

2 Chronicles 19:10

Ghadhabu itakuja juu yenu na juu ya ndugu zenu .

"Mungu atakuwa na hasira nanyi na ndugu zenu"

2 Chronicles 19:11

Amaria.

HIli ni jina la mtu mwanamme aliyekuwa kuhani mkuu.

Zabadia mwana wa Ishmaeli

Zabadia na Ishimaeli ni majina ya kiume.

2 Chronicles 20

2 Chronicles 20:1

Amoni.

Hili lilikuwa kundi la watu ambalo yawezekana liliishi karibu na Edomu, mashariki mwa mto Yorodani.

Hason-tamari.

Hili ni jina jingine la En-gedi.

2 Chronicles 20:3

Akajipanga.

"Alijidhatiti"

Kumtafuta Yahwe.

"Kujaribu kumtafuta Mungu ili awaangalie"

2 Chronicles 20:5

Yahwe, Mungu wa babu zetu, hauko mbinguni? Wewe siyo mtawala juu ya falme zote za mataifa?

"Hakika wewe ni Mungu wa mbinguni na mtawala juu ya wafalme wote wa dunia".

Nguvu na uweza viko mikononi mwako.

Maneno "nguvu" na "uweza" kimsingi yana maana moja na yanasisitiza ukuu wa nguvu za Yahwe. Neno "mkono" lina maana aya umiliki; "Una nguvu kuuu".

Hukuwafukuza nje wakaaji wa nchi hii mbele ya watu wako Israeli, na kuitoa milele kwa ajili ya uzao wa Abrahamu?

"Wewe ndidye uliwatoa nje watu waliokuwa wakiishi katika nchi hii kwa ajili ya watau wako Israeli na kuitoa milele kwa uzaoa wa Abraham"

2 Chronicles 20:8

Jina lako limo ndani ya nyumba hii.

"Uwepo wako umo ndani ya nyumba ahii".

2 Chronicles 20:10

Mlima Seiri

Hii ilikuwa sehemu ambapo Waedomu waliishi.

Ona jinsi wanavyotuzawadia; wanakuja kututoa nje ya nchi yako.

"Hivi ndivyo wanavyo 'tulipa' sisi kwa ajili ya huruma tuliyowaonesha; wanakuja kutufukuza nje ya nchi yako."

2 Chronicles 20:12

Hutawahukumu?

"Tafadhali wahukumu watu hawa"

Maacho yetu yako kwako.

"Tunakuangalia wewe kwa ajili ya amsaada"

2 Chronicles 20:14

Roho ya Yahwe ikaja juu.

Angalia sura ya 15:1

Yahazieli ... Zekaria ... Benaya ...Yeieli ... Matania ... Asafu.

Haya ni majina ya kiume (ni majina waliyoitwa wanaume).

2 Chronicles 20:16

Muende chini juu yao.

"Nendeni kwenye" au "nendeni mkapigane vita nao".

Njia ya Sisi.

Hili ni bonde jembamba liliko kati kati ya milima kusini mwa Yerusalemu.

Wokovu wa Yahwe.

Mungu atapigana vita na kuwaokoa watu wake.

2 Chronicles 20:18

Yuda wote.

"Watu wote wa Yuda"

Wakohathi na Wakorai.

Haya ni majina ya koo zilizokuwa katika Kabila la Lawi.

2 Chronicles 20:20

Tekoa.

Huu ulikuwa mji mmoja kusini mwa Yerusalemu.

Mtasaidiwa.

"Yahwe atawasaidia."

Amini katika amanabii zake, na mtafanikiwa.

"Kama amtaamini katika manabii wa Yahwe, basi mtafanikiwa."

2 Chronicles 20:22

Mlima Seiri

Angalia sura ya 20:10

Akapanga wanaume katika mavamizi.

"Akafanya mavamizi ya kusitukiza."

Ili kuwaua kabisa na kuwaangamiza.

Virai hivi viwili kimsingi vina maana moja. Cha pili kinatoa ufafanuzi wa kile cha kwanza. "Kuwaondoa kabisa".

2 Chronicles 20:24

Tazama, walikuwa wamekufa.

Hiki kilikuwa kitu cha kusitusha. Adui zao wote walikuwa wameuana wao kwa wao.

Walikuwa wamekufa, wameanguka chini.

Kirai "wameanguka chini" ni namna ya kusema kwamba "walikuwa wamekufa."wote walikuwa wamekufa ardhini."

2 Chronicles 20:25

Hata leo.

Angalia sura ya 5:9

2 Chronicles 20:27

Kila mtu wa Yuda na Yerusalemu.

Hii ni namna ya kusema kwamba kila mwanaume aendaye vitani.

Yehoshafati katika uongozi wao.

Mfalme Yehoshafati alikuwa mbele ya jeshi lote walipokuwa wakirudi Yerusalemu.

2 Chronicles 20:29

Hofu ya Yahwe ilikuwa juu ya falme zote za mataifa.

"Wafalme wote wa mataifa ya dunia wakamwogopa Mungu"

Falme.

Hii ina maana ya serikali zenye utawala mmoja.

2 Chronicles 20:31

Azuba, binti wa Shilhi.

Azuba ni jina la kike.

Akatembea katika njia za Asa.

"Aliufuata mfano wa Baba yake."

Akafanya yaliyo mema katika macho ya Yahwe.

Angalia suta ya 14:1

2 Chronicles 20:34

Mwana wa Hanani

Hanani ni jina la kiume.

Kitabu cha Wafalme wa Israeli.

Angalia sura ya 16:11

2 Chronicles 20:35

Meli

Hizi ni meli zenye uwezo wa kusafiri katika maji mengi.

Esion-geberi.

Angalia ssura ya 8:17

Maresha.

Angalia sura ya 11:5

Eliezeri.

Angalia sura ya 7:8, hili jina lile lile lakini la mtu mwingine tofauti na aliyetajwa katika mstari huo (7:8).

Dadavahu.

Jina la kiume.

2 Chronicles 21

2 Chronicles 21:1

Akalala pamoja na babu zake.

"Hii inamaanisha kwamba akafa" (Yehoshafati).

Mji wa Daudi.

Huu ni mji wa Daudi.

Azaria, Yerieli, Zekaria, Azaria, Mikaeli, na Shefatia.

Haya ni majina ya kiume; ni orodha ya majina ya watoto wa Yehoshafati mfalme wa Israeli.

Yehofati, mfalme wa Israeli.

Ufalme wa Kusini ulikuwa uknaitwa "Yuda", Llakini mwandishi wa kitabu hiki alitaka kuweka msistizo kwamba ufalme wa kusini ulikuwa katika hali ya kumtii Mungu, Israeli ya kweli.

Kiti cha enzi alimpa Yehoramu.

Yehoshafati aliamua kuwa Yohoramu awe mfalme baada yake (yaani akirithi kiti chake cha enzi).

2 Chronicles 21:4

Ameinuka katika ufalme wa baba yake.

"Amekuwa na mamlaka kamili juu ya ufalme wa baba yake."

2 Chronicles 21:6

Akatembea katika njia.

.Angalia sura ya 20:31.

Katika macho ya Yahwe.

"Kama Yahwe apendavyo"

Ameahidi kuwa siku zote atampa uhai yeye na kizazi chake.

"Ameahidi kuwa uzao wa Daudi siku zote watakuwa ndio watawala wa Yuda."

2 Chronicles 21:8

Katika siku za Yehoramu.

"Katika kipindi amacho Yehoramu alipokuwa mfalme."

Wakaasi wasiwe chini ya Yuda.

"Kinyume na mamlaka ya Yuda."

Akavuka ng'ambo.

"Akavuka mipaka kuingia Edomu."

Mpaka leo.

Angalia sura ya 5:9

Libna.

Huu ulikuwa mji katika Yuda.

2 Chronicles 21:11

Kahaba.

Neno "kahaba" lina maana aya mtu anayefanya kazi ya kujiuza kwa ajili ya kupata pesa au kwa mambo ya kidini. Kwa kawaida makahaba walikuwa wanawake, lakini wachache walikuwa wanaume.

2 Chronicles 21:12

Mpaka utumbo wako uanguke nje kwa sababu ya ugonjwa.

"Mpaka ugonjwa huu ukuuwe".

2 Chronicles 21:16

Akaichochea dhidi ya Yehoramu roho ya Wafilisti na ya Waarabu.

"Aliwasukuma Wafilisti na Waarabu

2 Chronicles 21:18

Yahwe akampiga katika utumbo wake kwa ugonjwa usiopona.

"Alimpiga ugonjwa usiotibika katika utumbo wake.".

Wakati ulipofika.

"Katika wakati sahihi" au "wakati sahihi ulipowadia".

Hawakutengeneza moto kwa ajili ya heshima yake.

"Hawakumheshimu kwa kwa moto mkubwa"

2 Chronicles 22

2 Chronicles 22:1

Athalia.

Athalia ni jina la kike.

Pia alitembea.

Angalia sura ya 20:31

2 Chronicles 22:4

Katika macho ya Yahwe.

"Katika matakwa ya Yahwe".

Hazaeli.

Hili ni jina la kiume(Ndilo jina aliloitwa mafalme wa Aramu ambayo ndiyo Ashuru).

2 Chronicles 22:7

Nimshi.

Nimshi ni jina la kiume.

2 Chronicles 22:10

Yehoshaba...Yehoiada.

Haya ni majina ya kiume.

2 Chronicles 23

2 Chronicles 23:1

Yehoyada.

HUyu ni kuhani mkuu aliyehudumu katika hekalu na kwa uaminifu kwa Mungu. Alikuwa mshauri wa Yoashi.

Obedi...Maaseya...Adaya...Elishafati...Zikri.

Haya ni majina ya Kiume

2 Chronicles 23:4

Watu wote.

Watu wengi.

2 Chronicles 23:6

Aingiapo ndani na atokapo.

Yaweza kuwa na maana hizi: 1) "Wakatai wote" au 2) Wakati wowote anapoenda".

2 Chronicles 23:8

Yuda wote walitumika kwa kila njia kama katika namna ambayo Yehoyada kuhanai aliwaamuru.

"Watu walio wengi walikuwa waaminifu katika amri za kuhani mkuu."

Wale watakaoondoka katika Siku ya Sabato.

"Waliokuwa wanamaliza kazi zao katika siku ya Sabatao."

2 Chronicles 23:10

Kumpa aganao la sheria.

"Aliyatamka maneno ya agano."

2 Chronicles 23:12

Watu wote wa nchi.

"Karibia watu wote."

2 Chronicles 23:14

Yehoyada

Yehoyada alikuwa kuhani

Waliokuwa juu ya jeshi.

Wale waliokuwa viongozi katika jeshi.

Kati ya safu.

Kati kati ya wanajeshi

2 Chronicles 23:16

Watu wote wakaenda kwenye nyumba ya Baali.

Karibu watu wote walienda kwenye hekalu la Baali.

Matani.

Huyu ni mtu mwanaume aliyeitwa Matani, alikuwa kuhani wa miungu ya Baali

2 Chronicles 23:18

Chini ya mkono wa Makuhani.

"Chini ya uongozi na maelekezo ya makuhani.

Ili kwamba kwa namna yoyote ile asiingie mtu asiye safi.

Hakuna mtu asiyesafi anaruhusiwa kuingia kwa sababu yoyoye.

2 Chronicles 23:20

Akamleta chini mfalme kutoka kwenye nyumba ya Yahwe.

Hekalu lilikuwa limejengwa juu ya mlima huko Yerusalemu. "Alimleta mfalme kutoka hekaluni kutoka juu ya kilele cha mlima hadi ikulu.

2 Chronicles 24

2 Chronicles 24:1

Sibia.

Jina la kiume.

Yaliyomema katika macho ya Yahwe.

Angalia sura ya 14:1

Siku zote za Yehoyada, yule kuhani.

"Muda wote wa maisha ya Yehoyada."

2 Chronicles 24:4

Mnaanza haraka.

"Haraka"

2 Chronicles 24:6

Kwa nini hukuwaagiza Walawi...amri za hema ya agano.

Mmetenda kwa uovu. Nilikuagiza kuwaagiza Walawi kuzifuata amri za hema ya agano, lakini kufanya hivyo.

2 Chronicles 24:11

Waashi na maseremala.

"Wale wajengao kwa mawe na wale wajengao kwa mbao."

walifanya kazi katika chuma na shaba.

"Wale waliokuwa wakifanya kazi kwa chuma."

2 Chronicles 24:13

Ikasonga mbele mikononi mwao.

"Walifanya kwa mikono yao."

Bia kukoma katika nyumba ya Yahwe kwa siku zote za Yehoyada.

"Kila siku kwa siku zote za maisha ya Yehoyada."

2 Chronicles 24:15

Akafa, kufa

Neno hili hutumika kumaanisha aina zote za vifo, yaani kifo cha kimwili na kifo cha kiroho. Kimwili, humaanisha kukoma kuisha katika mwili wa mtu. Kiroho humaanisha kitendo cha watu wennye dhambi kutengwa na Mungu mtakatifu kwa sababu ya dhambi zao.

Wakamzika, mazishi

Neno "zika" lina maaana ya kuweka mwili uliokufa katika shimo au sehemu ya kuzikia. na neno mazishi lina maana ya kitendo cha kuzika kitu fulani.

Mji wa Daudi.

Neno "mji wa Daudi" ni jina jingine la Yerusalemu na Bethelehemu. Yerusalemu ndiko alikoishi Daudi wakati akitawala Israeli. Bethelehemu ndiko alikozaliwa Daudi.

2 Chronicles 24:17

Kutoa heshima kwa mfalme.

"akatoa heshima kwa mfalme."

Hili kosa lao.

"kwa sababu ya dhambi zao."

2 Chronicles 24:20

Akapuuza ukarimu ambao Yehoyada, baba yake Zekaria alikuwa amemfanyia.

Yoashi hakujali wala kukumbuka ukarimu mkuu wa Yehoyada, baba yake Zekaria."

Akuite katika hukumu.

"Utalipa uovu ulioufanya."

2 Chronicles 24:25

Zabadi mwana wa Shimeathi, Mwamoni; na Yehozabadi mwana wa Shimrithi, Mmoabu.

Haya yote ni majina ya kiume.

2 Chronicles 24:27

Kamausi ya kitabau cha Wafaaalme.

Hiki ni kitabu ambacho kwa sasa hakipo tena.

2 Chronicles 25

2 Chronicles 25:1

Yehoadani.

Hili ni jina la mwanamke.

Yaliyokuwa sahihi katika macho ya Yahwe.

Angalia 14:1

2 Chronicles 25:3

Kitabu cha Musa.

Hii inarejea kitabu cha Mwanzo, Kutoka, Mambo ya Walawi, Hesabu, na Kumbu kumbu la Torati.

2 Chronicles 25:5

Akawaandikisha.

Liandika amajina yao katika orodha maalumu kwa ajili ya mambo ya kiofisi.

300,000...100.000

Laki tatu...Laki moja

Talanta.

Fedha

2 Chronicles 25:9

Hivyo Hasira yao iliwaka sana zidi.

"Kwa hiyo walianza kuwaka hasira."

Hasira kali.

"wakiwa na hasira sana."

2 Chronicles 25:11

Bonde la chumvi.

Hili ni Eneo karibu na Bahari iliyokufa.

Hivyo wote wakavujika vunjika katika vipande.

"Hivyo wote wakafa."

2 Chronicles 25:13

Beth-horoni.

Hili lilikuwa bonde lililokuwa kaaribu na Yerusalemu katika Efraimu.

Wakawapiga.

"Waliwaua."

2 Chronicles 25:14

Kuisimamisha iwe miungu yake.

"Wakaiabudu miungu hii ya uongo."

Kwa nini umeitafuta miungu ya watu ambayo haikuwaokoa hata watu wake yenyewe zidi ya mkono wako.

"Mmeiabudu miungu ya watu ambayo hata haikuweza kuwaokoa watu wake ddhidi yako, Mfalme Amazia.

2 Chronicles 25:16

Je, wewe tumekufanya msgauri wa mfalme? Acha.

"Kwa hakika hatukukuchagua kuwa mshauri. Kwa hiyo nyamazeni acheni kuszzungumza, na kama amtasema zaidi, nitawambia askari wangu kukuua.

Kwa nini ujitakie kuuawa?

Nitawaambia askari wangu wakuue.

2 Chronicles 25:17

Yehoashi, Yehoazi.

Haya ni majina ya kiume.

2 Chronicles 25:18

Taarifa za jumla:

Yehoashi alikuwa mfalme wa Israeli na Amaziahi alikuwa mfalme wa Yuda.

baruti.

Huu ni mstu mdogo.

Mwerezi.

Aina fulani ya mti mkubwa sana. Hapa neno hili linawakilisha wanajeshi au askari wa Israeli.

Kwa nini ujisababishie matatizo mwenyewe na kuanguka wewe na Yuda pamoja nawe?

"Hupaswi kujisababishaia matatizo mwenyewe na kujiangusha, wewe pamoja na Yuda."

2 Chronicles 25:20

Yuda walishindwa mbele za Israeli.

"Walishindwa."

2 Chronicles 25:23

Mikono.

Kipimo cha zamani

Obedi Edomu.

Hili ni jina la mtu.

2 Chronicles 25:25

Mwanzo na mwisho.

"kila kitu."

Hayajaandikwa katika kitabu cha wafaalme wa Israeli.

"Yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli."

2 Chronicles 25:27

Lachishi.

Hili ni jina la mji mmoja kataika Yuda.

Mji wa Yuda.

Ni jina jingine la mji wa Daudi, au Yerusalemu.

2 Chronicles 26

2 Chronicles 26:1

Kumi na sita...hamsini na mbili.

"16...52."

Elathi.

Huu ulikuwa mji mmoja ulikuwa akatika Ghuba ya Akaba.

Mfalme akalala pamoja na babu zake.

"Maana yake ni kwamba mfalme akafa."

2 Chronicles 26:4

Akafanya yaliyo sahihi katika macho ya Yahwe.

Angalia mstaraaisusra ya 14:1.

Katika kila kitu.

"Katika namna ile ile."

Alijitoa kumtafuta.

"Alijidhatiti kumpendeza."

2 Chronicles 26:6

Yabne.

Huu ulikuwa mji mmoja huko kaskazini mwa Yuda.

Gurbaali.

Huu ulikuwa mji mmoja huko Uarabuni.

Waamoni.

Huu ni ufalme wa watau wa Amoni karibu na Mlima Seiri.

Maingilio ya Misiri.

"Mipaka ya Misiri"

2 Chronicles 26:9

Mabwawa.

Katika mkitadha huu, bwawa nai shsimo kubwa chini ya ardhi ambalo lilitumika kuhifadhia maji ya mvua.

2 Chronicles 26:11

Yeieli, mwandishi, na Maaseya, afsa, chini ya mamlaka ya Hanania, mmoja wa maamri jeshi.

Maaseya na Hanania yote ni majina ya kiume.

2,600...307,500

Elfu mbili na na mia sita (2,600), Laki tatau na elfu saba na mia tano.

2 Chronicles 26:14

Chapeo.

Chapeo ni kitu kifaa cha kujilindia kinachofunika kichwa.

Deraya za majini.

Hili ni vazi la chuma linalofunika mwili mzima likiunganishwa na minyororo.

2 Chronicles 26:16

Moyo wake ulijiinua.

"Akawa na kiburi."

Wana wa Haruni.

"Uzao wa Haruni."

2 Chronicles 26:19

Chetezo.

Hil lilikuwa bakuli maalumu ambalo lilitumika kuchomea sadaka za kuteketezwa.

Walimwondoa pale haraka.

"Walimfanya ondoke haraka."

Yahwe alikuwa amempiga.

"Yahwe alimfanya augue."

2 Chronicles 26:21

Aliishi katika nyumba ya kutengwa.

Hii ina ashiria kuwa aliishi mbali na nyumba za watu wengine katika jamii au nchi.

2 Chronicles 26:22

Mwanzo na mwisho.

"Kila kitu."

Mwana wa Amozi.

Hili ni jina la kiume.

Kwa hiyo Uzia akalala pamoja na babu zake.

"Kwa hiyo Uzia akafa."

2 Chronicles 27

2 Chronicles 27:1

Yerusha.

Yerusha ni jina la kike.

Akafanya yaliyomema katika amacho ya Yahwe.

Angalia sura ya 14:1.

Katika mambo yote.

"Katika anamna ile ile."

2 Chronicles 27:3

Kilima caha Ofeli.

Hiki ni kilama kilichopo katika mji Yerusalemu.

2 Chronicles 27:5

Talanta.

Ainza ya fedha iliyotumika kataika siku au nyakati za Bilia.

Kori.

Kori kilikuwa kipimo kilichotumika katika siku za Biblia.

Katika mwaka wa pili na wa tatu.

"Katika mwaka wa pili na wa tatu baada ya kuwashinda."

2 Chronicles 27:6

Alitembea imara mbele za Yahwe Mungu wake.

"Alimtii Yahwe bila kuyumba" au "Aliishi kwa kujitoa kikamilifu kwa Yahwe."

Kitabu cha Wafalme wa Israeli na Yuda.

Hiki ni kitabu ambacho hakipo tena.

2 Chronicles 27:8

Yothamu akalala pamoja na babu zake.

"Yothamu akafa,"

2 Chronicles 28

2 Chronicles 28:1

Hakuafanaya aayaliyoadili katika macho ya Yahwe.

Angalia sura ya 14:1

Alitembea katika njia za wafalme wa Israeli.

"Alifanya dhambai kama vile walivyofanya wafalme wa Israeli waliomtangaualia."

2 Chronicles 28:3

Bonde la Beni Hinomu.

Hili ni bonde liloko katika Yerusalemu.

Chini ya kila mti wenye majani mabichi.

"Kila mahali au kila upande."

2 Chronicles 28:5

Peka mwana wa Remalaia.

Haya ni majina ya kiume.

2 Chronicles 28:7

Zikri...Maaseya...Azrikamu...Elkana.

Haya ni majina ya wanaume waliotajwa kwa kuhusika kwao katika matukio mbali mbali muhimu.

2 Chronicles 28:9

Odedi.

Odedi hili ni jina la amtu mmoja alikuwa nabii wa Yahwe au Mungu.

Akawatia katika mikono yenu.

"Aliwasaidia kuwashinda."

Lakini je, hamko na hatia...dhidi ya Yahwe Mungu wenu.

"Lakini kumbuka, ninyi ni wenye hatia...dhidi ya Yahwe Mungu wenu.

2 Chronicles 28:12

Azaria mwana wa Yohanani, Berikia mwana wa Meshiremothi, Yeehizikia mwa wa Shalumu, na Amasa mwana wa Hadlai

Hii ni ordha ya aamajina aya kiume aau ya wanaume ambao wlikwa viongozi wenye vyeo mbali mbali katika nchi ya Efraimu.

2 Chronicles 28:14

Viatu.

Hiii ilikuwa aina fulani ya viatu ambavyo vilikuwa vya wazi.

Wakawahudumia majeraha yao.

"Waliwapa huduma ya matibu."

Wakawaweka waliodhaifu juu ya punda.

"Wakawapa punda wale wasioweza kutembea."

2 Chronicles 28:16

Beth-shemeshi, Ayaloni, Giderothi, Soko pamoja na vijiji vyake, Timna pamoja na vijiji vyake.

Haya ni majina ya miji mbali mbali.

2 Chronicles 28:19

Yahwe aliishusha chini Yuda kwa sababu ya Ahazi.

"Yahwe alimnyenyekeza Ahazi."

Tiglath-pileseri.

Hii ni Tiglath-pileseri ya III, pia inajulikana kama Puli.

2 Chronicles 28:22

Katika muda wa mateso yake.

"Wakati wa mateso yake."

Nitawatolea sadaka.

"Nitawatolea sadaka ili wanisaidie."

2 Chronicles 28:24

Samani.

"Samani na vyombo vingine."

Katika kila kona ya Yerusalemu.

"Katika Yerusalemu."

2 Chronicles 28:26

Njia zake zote, mwanzo na mwisho.

"Kila kitu alichofanya."

Kitabu cha Wafalme wa Yuda na Israeli.

Hiki ni kitabu ambacaho hakipo tena.

Ahazi akalala pamoja na babu zake.

"Ahazi akafa."

2 Chronicles 29

2 Chronicles 29:1

Abiya.

Hili ni jina la kike (mwanamke)

Alifanya yaliyoadili katika macho ya Yahwe.

Tazama sura ya 14:1

2 Chronicles 29:3

Katika mwezi wa kwanza.

Huu ni mwezi wa kwanza katika Kalenda ya Kiebrania. Ni kati kati ya mwezi wa nne na wa nne katika kalenda ya Magharibi.

Uondoeni mbali uchafu.

"Ondoeni uchafu" au toeni uchafu."

2 Chronicles 29:6

Walikosea na kufanya kilichokuwa uovu katika macho ya Yahwe.

Angalia sura ya 21:6.

Sehemu ambapo Yahwe aliishi.

Angalia sura ya 18:12.

2 Chronicles 29:8

Wasi wasi, Hofu, kudharauliwa.

Haya yote ni maneno yanayoashiria kuwepo kwa hali mbaya ya kuogopa sana.

Kama aamnavyoona kwa macho yenu.

"Kama mnavyoweza kuona wenyewe."

Hii ndiyo maana mababu zetu walianguka kwa upanaga.

"Hivyo ndivyo baba zetu walivyouawa."

2 Chronicles 29:10

Ili kwamba hasira yake kali iweze kugeuka mbali nasi.

"Ili asikasirike na hasira yake iwe juu yetu."

2 Chronicles 29:12

Taarifa za jumla:

Haya ni majina ya watu wanaume kutoka Kabila la Lawi.

2 Chronicles 29:15

Kijito cha Kidroni.

Sehemu ndogo ya maji ambayo hutiririka upande wa mashariki wa Yerusalemu. Kuna wakati kijito hicho kilikuwa kikitumika kama jalala.

Siku ya kwanza ya mwezi.

Ni kipindi kilicho karibu na mwisho wa mwezi wa tatu katika kalenda ya magharibi.

Siku ya nane ya Mwezi.

Hiki ni kipindi cha mwanzo wa mwezi wa Nne kwa mjibu wa kalenda ya magaharibi.

2 Chronicles 29:18

Katika kipindi cha utawala wake.

"Katika kipindi cha utawala wake."

2 Chronicles 29:25

Matoazi.

Angalia sura ya 5:11.

2 Chronicles 29:31

Dhabihu za shukrani.

Hizi zilikuwa sadaka za shukrani.

Nani alikuwa na moyo wa hiari

"Aliyestahili"

2 Chronicles 29:32

Taarifa za jumla:

Hii ni idadi ya wanyama waliokuwa kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa.

2 Chronicles 29:34

Walikuwa makini sana kujitaksa wenyewe kuliko makuhani.

Walikuwa makini sana katika kufuata taratibu au sheria kwa ajili ya kujitakasa wenyewe.

2 Chronicles 29:35

Zilitolewa pamoja na sadaka za mafauta za amani.

Makuhani waliyachoma mafuta ya wanyama ambao walitolewa kama sadaka kwa ajili ya kulinda ushirika mzuri na Yahwe.

Ikawekwa katika utaratibu.

"Ziliimarishwa na makuhani kwa mjibu wa sheria"

2 Chronicles 30

2 Chronicles 30:1

Wakakubaliana kusherehekea Pasaka katika mwezi wa Pili.

Kwa kawaida Waisraeli walisherehekea Pasaka katika mwezi wa kwanza wa kalenda ya Kiebrania. Mwezi wa kwanza uko kati kati ya mwezi Machi na nusu ya kwanza ya mwezi Apirl Hii ni kwa mjibu wa kalenda ya magharibi.

Mwezi wa pili

Huu ni mwezi wa pili wa kalenda ya Kiebrania. Uko kati ya nusu ya pili ya mwezi Aprili na nusu ya kwanza ya mwezi Mei katika kalenda ya Magharibi.

2 Chronicles 30:4

Katika macho ya.

Tazama 14:1

Beer-sheba hadi Dani,

"Watu wote wa Israeli"

2 Chronicles 30:6

Matarishi.

Huyu alikuwa mtu aliyekuwa na kazi ya kupeleka ujumbe

2 Chronicles 30:7

Akawaweka katika uharibifu.

"Aliwafanya waangamie".

Jitoeni wenyewe kwa Yahwe

"Mtiini Yahwe" au jitoeni kwa ajili ya Yahwe".

2 Chronicles 30:13

Mwezi wa pili.

Huu ni mwezi wa pili katika kalenda ya Kiebrania. Ni mwezi ambao uko kati kati ya mwisho wa mwezi wa Apirl na mwazoni mwa mwezi Mei katika kalenda ya magharibi.

Kijito Kidroni.

Hii ilikuwa chemi chemi ya maji katika Bonde Kironi.

Siku ya kumi na na nnne ya mwezi wa pili..

Hiki ni kipindi karibu ya mwanzo wa mwezi wa Mei katika kalenda ya magharibi.

2 Chronicles 30:16

Wakasimama katika makundi yao.

Walisimama katika dhamu zao au sehemu zao walizopangiwa.

Wakawachinja wanakondoo wa Pasaka

Kwa kufuata desturi na taratibu waliwachinja wanakondoo wa Pasaka.

2 Chronicles 30:21

Vyombo.

Hii inarejea vyombo vya muziki.

2 Chronicles 31

2 Chronicles 31:1

Watu wote wa Israeli.

"Karibia watu wote wa Israeli."

2 Chronicles 31:2

Pia akawapanga katika sehemu ya mfalme kwa ajili ya sadaka kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kutoka katika mali zake.

Hezekia alichukua chalakua nyama na nafaka zilizokuwa zinatumika kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kutoka mali zake mwenyewe.

Mwezi mpya.

Hii ilikuwa sikukuu ambayo ilienda pamoja na hatua za mwezi.

Sikukuu zisizobadilika.

Hizi ni sikukuu ambazo hutokea katika tarehe maalumu.

2 Chronicles 31:4

Moja ya kumi ya kila kitu.

"Moja ya kumi ya mazao yao yote".

2 Chronicles 31:6

Mwezi wa tatu.

Huu ni mwezi wa tatu wa kalenda ya Kiebrania.Iko mwisho wa msimu wa mavuno na mwanzo wa msimu wa kiangazi.Ni mwisho wa mwezi wa tano na mwanzo wa mwezi Juni katika kalenda ya Magharibi.

Mwezi wa Saba.

Huu ni mwezi wa saba katika kalenda ya Kiebrania. Hiki ni kipindi cha msimu wa mvua za amwanzo, ambayo ilikuwa ikiilainisha nchi kwa ajili ya kupanda mazao. Ni mwishoni mwa mwezi Septemba na mwanzoni mwa Octoba katika kalenda ya Magharibi.

2 Chronicles 31:9

Kilichokuwa kimebaki ni kiasi kikubwa hiki hapa.

Kuhani mkuu alikuwa akisonta kwenye marundo makubwa.

2 Chronicles 31:14

Kore mwana wa Imna...Edeni, Miniamini, Amaaria, na Shekania

Haya ni majina ya kiume.

Chini yake.

"Chini ya mamlaka yake."

Wote walio muhimu na awsiomuhimu.

"Kila mmoja"

2 Chronicles 31:16

Umri wa miaka mitatu na kuendelea.

"Mika mitatu na zaidi"

Kwa mjibu wa aratiba ya kila siku.

Kama inavyotakiwa kila siku."

2 Chronicles 32

2 Chronicles 32:1

Matendo haya ya uaminifu.

Matendo haya yalifanywa na Hezekia.

2 Chronicles 32:2

Kuyazuia maji ya chemi chemi yaliyokuwa nje ya mji.

Walizifunga chemi chemi amabazo zilikuwa nje ya mji ili kwamba watu wasipate maji.

Kwa nini mfalme wa Ashuru aje na kupata maji mengi?

Mfalme wa Ashuru hapaswi kuja na kukuta mengi. Wakalimani wanaweza kusema "mfalme wa Ashuru", kwa sababu hakuna kifunga cha kurejea na kupa masaada wa taarifa za mfalme.

2 Chronicles 32:5

Akajipa ujasiri.

Angalia sura ya 15:8.

Hezekia akajipa ujasiri na kujenga.

"Hezekia alijipa moyo mwenyewe na watu na wakajenga."

Milo.

Hii sehemu ya ukuta amabayo inaushikilia ukuta na kuufanya kuwa imara.

2 Chronicles 32:6

Kwa maana kuna mtu yuko pamoja nasi ambaye ni mkuu kuliko waliye naye mfalme wa Ashuru

"Kwa maana Mungu wetu yuko nasi, tena ananguvu kuliko wao."

Jeshi la mwili.

"Nguvu za kibinadamu."

2 Chronicles 32:9

Lakishi.

Huu ulikuwa mji katika Yuda.

Ni kitu gani mnategemea kwa ajili ya kuhimili uvamizi katika Yerusalemu.

"Hamna uwezo wwa kuhimili uvamizi unaokwenda kutokea katika Yerusalemu."

2 Chronicles 32:11

Je, Hezekia hawapotoshi ninyi ... anapowaaambia, 'Yahwe ...Ashuru'?

"Hezekia anawapotosha ninyi... anapowaamaabia, 'Yahwe atatuoko na mkono wa mfalme wa Ashuru."

Je, siyo Hezekia yule yule ambaye amezipeleka juu sehemu zake na madhabahu zake ...

"Ni Hezekia yule yule aliyefanya hivyo."

2 Chronicles 32:13

Je, hamjui mimi na babu zangu tulifanya nini kwa makundi ya watu wote wa nchi zingine?

"Mnajua vyema sana."

Je, miungu ya watu wa nchi hizo iliweza kwa njia yoyote iliweza kuziokoa nchi zao dhidi ya nguvu zangu?

"Miungu ya makundi ya watu wa nchi hizo kamwe haikuweza kuwaokoa watu wake dhidi ya nguvu zangu!"

Miongni mwa nchi hizo zote, je kulikuwa na miungu iliyoweza kuwaokoa watu wake kutoka kwenye mkono wangu?

"Hapakuwa na muungu kati ya miungo yote ambaye aliweza kuwaokoa!"

Itakuwaje Mungu wenu ninyi aweze kuwaokoa ninyi dhidi ya nguvu zangu?

"Hakuna sababu ya Mungu wenu kuweza kuwaokoa ninyi dhidi ya mkono wangu!"

2 Chronicles 32:18

Ili kuwaogopesha na kuwasumbua.

Virai hivi viwili vina maana ya kitu kimoja na vinasisitiza swala la hofu ("kuwafanya waogope sana.")

Wakamnenea Mungu wa Yerusalemu kama walivyowanenea miungu wa Dunia.

"Wakamdhihaki Mungu wa Yerusalemu kama walivyokuwa wamewadhihaki miungu wa watu wengine wa Dunia."

2 Chronicles 32:20

Wakalia hadi mbinguni.

"Wakamsihi Mungu."

Uso wa aibu.

"Akiwa ameaibika" au "mwenye aibu."

Nyumba ya muungu wake.

"Hekalu la muungu wake."

2 Chronicles 32:22

Akawapa pumziko katika kila upande

"Mahali hapa "pumziko" linamaana ya "amani". Aliwapa amani pamoja na watu wa nchi zingine jirani.

Mbele za macho ya mataifa yote.

"Kwa hiyo watu wote jirani wakajua"

2 Chronicles 32:24

Moyo wake uliinuliwa juu.

"Akajivuna"

2 Chronicles 32:27

Malisho.

Angalia sura ya 9:25

Pia alikuwa na makundi katika mazizi.

Sehemu ya kuhifadhia kwa ajili ya wanyama wadogo wadogo.

2 Chronicles 32:30

Maji ya Gihoni.

Gihoni ni jina la mahali ampapo palikuwa na chemi chemi za maji

2 Chronicles 32:32

Maono ya Nabii Isaya Mwana wa Amozi...na katika kitabu cha wa Yuda na Israeli.

Vitabu hivi havipo tena.

Hezekia akalala pamoja na babu zake.

Rejea sura ya 9:29

2 Chronicles 33

2 Chronicles 33:1

Akafanya yaliyokuwa uovu katika macho ya Yahwe.

Rejea sura ya 14:1

Kama yalivyo mambo ya machukizo ya mataifa ambayo Yahwe alikuwa amewafukuza mbele ya watu wa Israeli.

"Kama alivyowatendea watu wengine ambao Yahwe aliwasababisha kupigwa na watu wa Israeli".

2 Chronicles 33:4

Jina langu litawekwa.

"Nitajifanya mwenyewe nijulikane kwa watu"

Akawaweka wanaye katika moto.

"Hiki kilikuwa kitendo cha kuwachoma watoto katika moto kama wakiwa hai kama sadaka kwa miungu"

Bonde la Beni Hinomu

Hii ni sehemu iliyopo karibu na Yerusalemu ambayo pia inajulikana kama Jehena.

2 Chronicles 33:7

Yuda na wakaaji wa Yerusalemu.

"Watu wa Yuda na Yerusalemu".

2 Chronicles 33:10

Akaleta juu yao.

"Akaleta mavamizi juu yao"

2 Chronicles 33:12

Akaomba kwake; na Mungu akasikia kuoma kwake

"Kirai cha pili kina weka msistizo wa kirai cha kwanza na kinasistiza kuhusu maombi ya Manase. "Alimwomba na kumsihi Mungu."

2 Chronicles 33:14

Maelezo ya jumla .

Manase alikuwa mfalme wa Yuda, ndiye aliyewasababisha watu wa Yuda na Yerusalemu kufanya uovu mbele za macho ya Yahwe.

Miungu ya kigeni.

"Miungu ya uongo kutoka nchi zingine."

2 Chronicles 33:16

Akamwamuru Yuda.

"Aliwaamurisha watu wa Yuda."

2 Chronicles 33:18

Yameandikwa miongoni mwa wafalme wa Yuda.

Tukio hili katika historia ya Israeli halipo tena.

Tarehe ya waonaji.

Hiki ni kitabu ambacho hakipo tena.

Kwa hiyo Manase akalala pamoja na babu zake, na walimzika pamoja nao.

"Kwa hiyo Manase akafa, na familia yake wakamzika".

Amoni.

Hili ni jina la kiume.

2 Chronicles 33:21

Akafanya yaliyokuwa uovu katika macho ya Yahwe.

Angalia sura ya 14:1.

Amoni huyu huyu alifanya makosa zaidi na zaidi

"Amoni alitenda dhambi zaidi"

2 Chronicles 33:24

Wakapanga njama

"Wakapanga kwa mpngo kwa siri."

2 Chronicles 34

2 Chronicles 34:1

Alifanya yaliyo haki katika macho ya Yahwe,

Angalia sura ya 14:1

Hakugeuka mbali iwe kulia au kushoto.

"Hakusita kumtii Mungu katika hali yoyote", au "alitii amri zote za Mungu"

2 Chronicles 34:4

Hadi zikawa mavumbi.

Hadi zilipokuwa vipande vidogo vidogo sana kiasi cha kuweza kuchukuliwa na upepo".

2 Chronicles 34:6

Kuwa unga.

"Zile sanamu aliziharibu kabisa zikaisha au zikateketea"

2 Chronicles 34:8

Maelezo ya jumla.

Yosia ni jina la mtu mwanamme, huyu alikuwa mfalme.

Wakakabidhi kwake.

"Walimpa yeye jukumu la kusimamia matumizi ya fedha hizo."

2 Chronicles 34:10

Waliziacha zikaanguka

"Waliziruhusu zikaharibika."

2 Chronicles 34:12

Taarifa za jumla.

Haya ni majina ya watu kutoka koo mbali mbali za Kilawi.

Walawi hawa walikuwa viongozi wa wale waliobeba vifaa vya ujenzi na watu wengine wote waliofanya kazi kwa namna yoyote ile.

"Walawi hawa walikuwa wasimamizi au viongozi wa wanaume wote waliokuwa wakifanya aina zote za kazi za ujenzi."

2 Chronicles 34:14

Taarifa za jumla:

Hilkia alikuwa kuhani na Shefank alikuwa mwandishi, yaani mtu aliyekuwa na kazi ya kuandika mambo mbali mbali yamhusuyo Mungu.

Walipoileta fedha ambayo ilikuwa imeletwa kwenye nyumba ya Yahwe.

"Wasimamizi walipokuwa wanaipokea fedha kwenye hekalu"

Watumishi wak wanafanya kila kitu walichokabidhiwa.

"Kila kitu ambacho uliwapa jukumu la kukifanya"

2 Chronicles 34:17

Waliitoa fedha yote.

"Walikuwa wameikusanya"

Ikawa kwamba.

Kirai hiki ni alama; kina onesha au kuashiria kwamba tukio au jambo linalofuata katika hadithi hii ni muhimu sana; ni sawa na kusema, "Sasa, tambua kinachofuata".

2 Chronicles 34:20

Taarifa za jumla:

Hii ni ordha ya majina ya makuhani na watumishi mbali mbali wa mfalme katika nhyumba ya Mungu kwa wakatai huo.

Mkaulize mapenzi ya Yahwe kwa ajili yangu.

"Maulize ili mjue ambacho Yahwe anataka nifanye".

"Kwa sababu ya maneno ya kitabu"

"Kwa mjibu wa yale yaliyoandikwa katika kitabu"

Kwa maana ni kikuu, gadhabu ya Yahwe ambayo imemiminwa juu yetu. Ni kuu.

Aina ya hisia kama gadhabaau au hasira huzungumzwa kama kimiminika; kwa kuwa gadhabu ya Yahwe dhidi yetu ni kuu, kama vile maji ambayo yanauwezo wa kuosha kabisa na kutufutilia mbali".

2 Chronicles 34:22

Taarifa za jumla:

Hilkia ni miongoni mwa watumishi wa mfalme

Mtunza mavazi.

"Mtu aliyekuwa na kazi ya kutunza mavazi au kanzu za kikuhani"

Walizunguza naye katika namna hii

"Walifanya naye maongezi yafuayo."

2 Chronicles 34:23

Ili kwamba waniweke katika hasira kwa matendo yao waliyofanya.

"Matokeo yake ni kwamba wamenifanya nikasirike sana kwa sababu ya yale waliyofanya"

Kwa hiyo hasira yangu itamiminwa ajuu ya hii sehemu ,na haitazimishwa.

Aina hii ya hisia kama hasira mara zote katika maandiko huzungumzwa kama vile kimiminika; "kwa hiyo itakuwa kama moto unaomiminwa juu yao, na hakuna kitu kitakachoweza kuuzima moto huu"

2 Chronicles 34:26

Yahwe, Mungu wa Israeli anasema hivi: kuhusu maneno uliyoyasikia, kwa sababu ya moyo wako ulipondeka.

" Yahwe, Mungu wa Israeli anasema hivi kuhusu maneno uliyoyasikia, kwa sababu moyo wako ulipondeka -ukakubali kubadilika".

.Umeyalarua mavazi yako.

Hii ilikuw ishara ya hudhuni na toba.

Nitakukusanya pakwa babu zako. Utakusanywa katika kaburi lako kwa amani.

"Utakufa."

Macho yako hayataona.

"Hautaonja au kusshudia."

2 Chronicles 34:29

Watu wote kuanzia wakubwa hadi wadogo.

"Kila mtu."

Akasoma mbele zao.

"Akawasomea."

2 Chronicles 34:31

Akisimama katika sehemu yake.

Akasimama mahali alipopaswa kusimama kwe lango la kuingia hekaluni"

Kwa moyo wake wote na roho yake yote.

Kwa pamoja, maneno haya mawili yanatoa maana inayohusu utu mzma wa mtu au utu wote wa mtu.

Wote walioonekana katika Yerusalemu na Benyamini.

"Wote waliokuwa wakiishi katika Yerusalemu na Benyamini."

2 Chronicles 34:33

Mambo yote ya machukizo

Hii ilikuwa ni miungu ambayo ilileta machukizo mbele za Mungu.

2 Chronicles 35

2 Chronicles 35:1

Siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza.

Huu ni mwezi wa kwanza wa kalenda ya Kiebrania. Mwezi wa kumi na nne uko karibu ya ya mwanzo wa mwezi Apirl katika kalenda ya maghari.

Akawaweka makuhani katika nafasi zao.

"Aliwaambia makuhani kuhusu kazi za kufanya".

2 Chronicles 35:3

Ambayo Selemani mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli aliijenga.

"Watu waliijenga nyumba hiyo chini ya uongozi wa Mfalme wa Selemani"

Kwa majina ya nyumba za mababu zenu na zamu zenu.

"Kabila zenu na familia zenu"

2 Chronicles 35:5

Simameni katika sehemu takatifu.

Hapa "sehemu takatifu" zinaonekana kutaja maeneo mbali mbali ya hekalu. "kaeni katika zamu zenu katika hekalu"

Zamu zenu.

Hii inataja kundi la kazi lililopangwa kwa kila Mlawi.

Nyumba za mababu.

Hizi ni koo mbali mbali miongoni mwa Walawi. Inaonekana kwamba Walawi walikuwa wamepangiwa makundi ya kazi mbali mbali kwa kuzingatia aina ya kazi iliyokuwa imepangwa kwa kila ukoo au nyumba ya mababu.

2 Chronicles 35:7

Taarifa za jumla:

Yosia ni jina la mwanaume aliyekuwa mfalme. Majina mengine katika kifungu hiki ya wanaume mbali mbali ambao walikuwa viongozi au wasimamizi katika nyumba ya Yahwe, pia kuna majina ya watu wengine kama makuhani kutoka kabila la Lawi.

Wanambuzi.

Huyu ni mtoto wa mbuzi.

2 Chronicles 35:10

Huduma iliandaliwa.

"Walitayarisha kila kitu kwa ajili ya kuifanya Pasaka"

Damu waliyoipokea kutoka kwenye mikono ya Walawi.

"Damu ambayo Walawi waliwapa."

2 Chronicles 35:13

Wakawaoka kwa moto.

"Waliwapika"

Walizichemsha kwenye vyungu, masufuria, na makaangoni kwa ajili yao wenyewe.

"Waliwapika kataika maji katika vyungu mbali mbali."

2 Chronicles 35:15

Taarifa za jumla:

Haya ni majina ya wanaume ambao walikuwa na huduma au kazi maalumu kama vile ukuhani na unabii.

Katika nafasi zao.

Angalia sura ya 30:16.

2 Chronicles 35:16

Huduma yote.

Kila kitu kilichohusiana na maandalizi ya sadaka na ibada ya Yahwe wakati wa pasaka yanaweza kuwa na maana ya huduma ya ibada.

2 Chronicles 35:18

Israeli

Maana ya kwanza ya neno Israeli lina wakilisha taifa zima la Israeli, lakini maana ya pili ya neno hili Israeli linataja au linawakilisha makabila ya kaskazini ya ufalme wa Israeli.

2 Chronicles 35:20

Taarifa za jumla:

Neko alikuwa mfalme wa Misri na alichukuwa uamuzi wa kwenda kupigana vita na Yosia , mfalme wa Yuda.

Kuliweka hekalu katika utaratibu.

"Alirejesha ibada yenye utaratibu mzuri katika hekalu"

Nikufanye nini, mfaalme wa Yuda?

"Huna sababu ya kunivamia mimi wewe Mfalme wa Yuda".

Mimi iiji kinyume nawe.

"Mimi ssipigani wala kupingana na ufalme wako".

Lakini dhidi ya nyumba ambayo nafanya vita nayo.

"Dhidi ya Babeli. dhidi ya ya wale ninaofanya vita nao".

2 Chronicles 35:22

Apigane naye.

"Apigane na jeshi la Wababeli"

Ambayo yalikuja kutoka kwenye kinywa cha Mungu.

"Kutoka kwa Mungu" au ambayo Mungu alikuwa amemwambia"

2 Chronicles 35:25

Hata leo

Angaalia sura ya 5:9

2 Chronicles 36

2 Chronicles 36:1

Yehoazi.

Huyu alikuwa mwana wa kiume wa mfalme Yosia, watu walimchukua na kumfanya mfalme

2 Chronicles 36:3

Taarifa za jumla

Eliakimu alikuwa ndugu wa mfalme wa Misri na ndiye alifanywa kuwa mfalme wa Yuda.

Talanta.

Fedha ya zamani (talanta moja ilikuwa sawa na vito vya thamani vyenye uzito upatao kilo 33.

Kumpeleka Misri.

"Akampeleka Misiri kama mfungwa".

2 Chronicles 36:5

Akafanya ambayo yalikuwa maovu katika macho ya Yahwe.

Angalia sura ya 21:6

Akamvamia.

Nebukadreza aliuvamia Yerusalemu.

Nebukadreza pia akpeleka baadhi ya vitu.

Watumishi wa Nebukadreza walichukua vitu katika nyumba ya Yahwe na kuvipeleka Babeli.

2 Chronicles 36:8

Mambo mabaya ambayo aliyafanaya.

Kwa kawaida hii ina maana aya kuabudu miungu ya uongo, ambayo Yahwe aliichukia.

Yaliyopatikana dhidi yake.

Hii inaweza kuwa inataja au kuelezea tabia yake

Kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.

Angalia suya ya 35:2

2 Chronicles 36:9

Akafanya yaliyokuwa maovu katika macho ya Yahwe.

Angalia sura ya 14:1

2 Chronicles 36:11

Hakujinyenyekesha mwenyewe mbele za Yeremia nabii.

"Hakujinyenyekesha mwenyewe na kumtii Mungu kwa kumsikiliza nabii Yeremia "

Kutoka kwenye kinywa cha Yahwe.

"Kutoka kwenye maneno ambayo Mungu alikuwa amempa."

2 Chronicles 36:13

Aliishupaza shingo yake na kuufanya moyo wake mgumu.

Haya ni maneno mawili yanayotoa namna mbili za kuutaja usumbufu au ugumu wa moyo wa mtu. Kwa pamoja yanasisitiza uasi wa Sedekia dhidi ya Mungu.

Waliigoshi nyumba ya Yahwe.

"Walikitia unajisi kile ambacho kilipaswa kuwa kitakatifu"

2 Chronicles 36:15

Tena na tena

"Nyakati nyingi"

Palikosekana msaada.

Hapakuwa na namna ya kuizuia hasira ya Yahwe.

2 Chronicles 36:17

Mungu akawatoa wote mkononi mwake.

"Mungu akaruhusu jeshi la Wakaldayo kuwashida au kuwapiga"

2 Chronicles 36:18

Akavipeleka.

Askari wake walivichukua vyombo

Wakaichoma moto

"Wakaichoma" inawataja askari wa Kibabeli.

2 Chronicles 36:20

Mfalme akawapeleka.

"Askari wa mfalme waliwachukua"

2 Chronicles 36:22

Katika mwaka wa kwanza

Katika mwaka wa kwanza (1)

Ameniagiza nijenge nyumba

"Amenichagua ili niwaamuru watumishi wangu wamjengee hekalu katika Yerusalemu"

Ezra 1

Ezra 1:1

mwaka wa kwanza

inarejea mwaka wa kwanza wa kutawala mfalme Koreshi

Yahwe

Hili ni jina la Mungu ambalo alilifunua kwa watu wake katika agano la kale. Angalia neno la tafsiri kwenye ukurasa unaouhusu Yahwe kuhusiana na jinsi ya kutafsiri.

Yahwe akatimiza neno lake

"Yahwe akafanya kile alichokisema kuwa atakifanya"

ambalo lilikuja kwa kusemwa na Yeremia

Ambacho Yeremia alikiandika au kukiongea kuhusu.

Yahwe..... kuinua roho ya Koreshi

Kuinua roho ni msemo wa kumfanya mtu atake kutenda "Yahwe .....akamfanya Koreshi atake kutenda"

Sauti ya Koreshi ikasambaa kote kwenye ufalme wake

Sauti ni aina msemo wa ujumbe sauti inaongea, na ufalme ni msemo kwa watu ambao mfalme anawaongoza. AT: "Koreshi akatuma ujumbe kwa kila mmoja ambao anawaongoza"

Kitu gani kiliandikwa na kuongelewa

Hii inaweza kutafsiriwa kwa mfumo hai. Itakuwa vizuri kutafsiri ili kwamba wasomaji waelewe kwamba watu wengine walimsaidia Koreshi kupata ujumbe kwa watu ambao anawaongoza. AT:"Kile alichokiandika Koreshi na kile wajumbe wake walikisoma ili watu waweze kuwasikia wao"

Ufalme wote wa dunia

Hii ni kukiuka, kana kwamba kulikuwa na ufalme ambao Koreshi alikuwa hauongozi

kwa yeye nyumba katika..... Yuda

Ungependa kufanya........... kwamba nyumba ilikuwa kwa ajili ya watu kumwabudu Yahwe. AT:"nyumba katika....... Yuda ambapo watu wanaweza kumwabudu yeye"

Ezra 1:3

watu wake

watu walio katika umiliki wa Yahwe

waliosalia katika nchi........ walipaswa kuwapa wao

Wale waisraeli waliochagua kubaki pale walipo walipaswa kuwasaidia wale waliochagua kwenda Yerusalem kimwili na kiuchumi.

Ezra 1:5

kazi zao

Hii inarejea kazi ya watu katika mstari uliopita iliyohimizwa na Mungu.

kila mmoja ambaye roho wa Mungu alimwinua kwenda

Kuinua Roho ni msemo kwa kumfamya mtu atake kufanya. AT: "kila mmoja ambaye Mungu alimfanya aweze kwenda"

Ezra 1:7

Mithredathi......... Sheshbaza

Haya ni majina ya wanaume

akaviweka katika mikono ya Mithredathi mtunza fedha

Kuweka kitu katika mikono ya mtu ni fumbo la kumruhusu mtu kufanya kile anachotaka kwa kitu ulichompa. Hapa wasomaji waelewe kwamba Koreshi alitegemea Methredathi kufanya ambacho Koreshi alimtaka akifanye.AT:"kumweka Methredathi mtunza fedha kiongozi wao" au "kumweka Methredathi mtunza fedha kuwajibika kwa ajili yao"

mtunza fedha

kiongozi mhusika wa fedha

akavitoa na kuvihesabu kwa Sheshbaza

kuhakikisha kwamba Sheshbaza anafahamu kwa uhakika vitu vyote vilivyo

Ezra 1:9

Taarifa kwa ujumla

Hii ni orodha ya idadi ya vitu

Therasini ....... moja elfu....... ishirini -tisa

tisa - "30..... 1,000.... 29"

beseni......mabakuli

vyombo vilivyotumika kutunzia maji ya kunawia

5,400 dhahabu na vitu vya fedha vyote

jumla ya idadi ya vitu vilivyorudi Yerusalem kutoka Babeli, vimeorodheshwa hapo juu kwa kutenganishwa.

Ezra 2

Ezra 2:1

Taarifa kwa ujumla

Hii ni mwanzo wa orodha ya majina ya watu waliorudi kutoka mateka

kwenda

Hii ni idom ambayo inarejea kutembea kuelekea Yerusalem. AT:"kurudi" au "kurudi tena"

Seraya,Reelaya,Mordekai,Bilshani,Mispari,Bigwai,Rehumu na Baana

Haya ni majina ya wanaume

Ezra 2:3

Taarifa kwa ujumla

Hii inaendelea na orodha ya majina ya watu waliorudi kutoka mateka pamoja na idadi ya kila kundi

Paloshi..... Shefatia..... Ara.....PathMoabu...... Yeshua

Haya ni majina ya wanaume

Ezra 2:7

Taarifa kwa ujumla

Hii inaendelea na orodha ya majina ya watu ambao walirudi kutoka mateka pamoja na idadi ya kila kikundi

Zatu....Zakai......Binui

Haya ni majina ya wanaume

Ezra 2:11

Taarifa kwa ujumla

Hii inaendelea na orodha ya majina ya watu ambao walirudi kutoka mateka pamoja na idadi ya kila kikundi

Bebai.....Azgadi......Adonikamu

Haya ni majina ya wanaume

Bigwai

jina la mtu tafsiri kama ulivyofanya katika 2:1

Ezra 2:15

Taarifa kwa ujumla

Hii inaendelea na orodha ya majina ya watu ambao walirudi kutoka mateka pamoja na idadi ya kila kikundi

Adini....Ateri........Besai

Haya ni majina ya wanaume

tisini-nane

nane "98"

Ezra 2:19

Taarifa kwa ujumla

Hii inaendelea na orodha ya majina ya watu ambao walirudi kutoka mateka pamoja na idadi ya kila kikundi

Hashimu.....Gibeoni

Haya ni majina ya wanaume

tisini-tano.......hamsini-sita

tano........hamsini-sita - "95......56"

Wanaume wa Bethlehemu

Hii inaanza orodha ya idadi ya watu ambao watangulizi wao waliishi katika mji wa Yuda

Netofa

Hii ni jina la mji katika Yuda

Ezra 2:23

Taarifa kwa ujumla

Hii inaendelea na orodha ya watu ambao walirudi kutoka mateka pamoja na idadi ya kila kikundi ambao watagulizi walikuja kutoka sehemu zilizo orozeshwa

Anathothi.....Azmawethi....Kiriath- Yearimu....Kefira.......Beeerothi......Geba

majina ya maeneo

arobaini - mbili

mbili - "42"

Ezra 2:27

Taarifa kwa ujumla

Hii inaendelea pamoja na idadi ya watu ambao walirudi kutoka mateka pamoja na idadi ya kila kikundi ambao watangulizi walikuja kutoka sehemu zilizoorodheshwa.

Mikmashi.....Nebo..Magbishi

majina ya maeneo

hamsini-mbili

mbili - "52"

Ezra 2:31

Taarifa kwa ujumla

Hii inaendelea na orodha ya watu ambao walirudi kutoka mateka pamoja na idadi katika kila kikundi ambacho watangulizi walikuja kutoka maeneo yaliyo orodheshwa

Harimu.....Lodi......Hadidi........Ono

majina ya maeneo

Ezra 2:34

Taarifa kwa ujumla

Hii inaendelea pamoja na idadi ya watu ambao walirudi kutoka mateka pamoja idadi katika kila kikundi ambao watangulizi walikuja kutoka maeneo yaliyo orodheshwa

Senaa

majina ya maeneo

Ezra 2:36

Taarifa kwa ujumla

Sehemu hii inaorodhesha majina ya makuhani ambao wana wao walirudi kutoka matekani pamoja na idadi ya kila kikundi.

Yedaya.....Imeri.......Pashuri......Harimu

majina ya wanaume

Yeshua

jina la mtu

Harimu

Harimu 2:31 ni jina la eneo, lakini hapa "Harimu" ni jina la mtu

Ezra 2:40

Taarifa kwa ujumla

Hii sehemu inaonyesha idadi ya majina ya Walawi ambao wanao walirudi kutoka mateka pamoja na idadi ya kila kikundi

Kadmiel...Hodavia...Shalumu...Talmoni,Akubu,Hatita, na Shobai

majina ya wanaume

Sabini na nne

nne "74"

walinzi

wale wahusika ambao huenda kupitia geti la Hekalu

Ateri

jina la mtu

Ezra 2:43

Taarifa kwa ujumla

Hii sehemu inaendelea kuoorodhesha majina ya Walawi ambao wanao walirudi kutoka mateka .

Siha,Hasufa,Tabothi,Keros,Siaha,Padoni,Hagaba...Hagaba,Salmai, na Hanani

majina ya wanaume

Akubu

Tafsiri kama ilivyo katika 2:40

Ezra 2:47

Taarifa kwa ujumla

Hii sehemu inaendelea kuorodhesha majina ya Walawi ambao wanao walirudi kutoka mateka. Haya ni majina yote ya wanaume

Ezra 2:51

Taarifa kwa ujumla

Hii sehemu inaendelea kuorodhesha majina ya walawi ambao walirudi kutoka mateka.Haya ni majina yote ya wanaume

Ezra 2:55

Taarifa kwa ujumla

Hii sehemu inaendelea kuoorodhesha majina ya Walawi ambao wana wao walirudi kutoka mateka

walikuwa wapatao 392 jumla ya wana

Hii ni idadi ya watu wote katika hili kundi ambao walirudi kutoka mateka

Ezra 2:59

Taarifa kwa ujumla

Hii ni orodha ya watu ambao walirudi Israeli kutoka baadhi ya miji ya Babeli lakini hawakuweza kuthibitisha kizazi chao.

Tel-mela,Tel charsha,Kerubu,Adani,na Imeri

ni maeneo katika Babeli ambayo hayapo kwa sasa.

Delaya,Tobia, na Nekoda

majina ya wanaume

Ezra 2:61

Habaya....Hakosi....Barzilai

majina ya wanaume

kumbukumbu ya kizazi chao

kumbukumbu ambayo ilielezea watangulizi walivyokuwa

hawakuweza kupatikana

"hawakuweza kuyaona majina yao katika kumbukumbu ya makuhani"

waliweza kutolewa kutoka kwa makuhani kama wasiosafi

Hii inaweza kutafsiliwa katika mfumo hai. Majina "Ukuhani" linaweza kutafsiliwa kama kitenzi "kazi kama ya kuhani." AT: makuhani wengine waliwachukulia wao kama wasio safi hawakuwaruhusu kufanya kazi kama makuhani"

wasiosafi

kutokuwa sawa kuwa kuhani

Urimu na Thumimu

vitu viwili kama dai ambavyo kuhani alivitumia kuamua kitu gani ambacho Mungu anataka wao wakifanye

Ezra 2:64

kundi lote

kundi lote ambalo lilirudi tena kwenye ardhi ya Yuda kutoka mateka

wasaidizi wao

"watumishi wao wa kike"

mia mbili

"200"

Ezra 2:66

Taarifa kwa ujumla

Hii ni orodha ya wanyama pamoja na idadi ya kila aina ambao walirudi pamoja na watu kutoka mateka.

Ezra 2:68

sitini-moja elfu...elfu tano...elfu moja

elfu moja...elfu tano...mia moja "61,000...5,000...100"

dhahabu za darkoni

"darkoni" ilikuwa ni salafu ndogo ya dhahabu iliyotumika katika utawala wa uajemi

mane

Mane ni kipimo cha uzito. mane moja ni sawa na gramu 550. mane kawaida ilihusishwa na vipimo vya fedha.

mavazi

mavazi yaliyovaliwa juu ya ngozi

Ezra 2:70

watu wote katika Israeli walikuwa katika miji yao

Kila mmoja alirudi tena kwenye mji wa nyumbani Yuda. Si kila mmoja alikaa katika Yerusalem.

Ezra 3

Ezra 3:1

mwezi wa saba

huu ni mwezi wa saba katika kalenda ya kiebrania.Ni kipindi cha mwisho cha kiangazi na mwanzoni mwa nyakati za mvua. Ni kipindi cha mwisho cha mwezi wa tisa na kipindi cha mwanzo wa mwezi wa kumi kwa kalenda ya watu wa magharibi.

kama mtu mmoja

mtu mmoja yuko katika sehemu moja na ana kusudi moja. AT: "kwa kusudi moja"

Yeshua

Hili ni jina la mtu.Litafsiri kama katika 2:36

Sheatieli

Hili ni jina la mtu.

kuinuka na kujenga

Kuinuka juu ni msemo wa kuanza kutenda. AT: "kuanza kutenda na kujenga"

kama ilivyoamliwa katika sheria ya Musa

Hii inaweza kutafsiriwa katika mfumo hai. Unatakiwa kufanya kile ambacho Yahwe alikiagiza. AT: "kama vile Yahwe alivyoagiza wao wafanye kama vile sheria ya Musa"

Ezra 3:3

wakaanzisha nadhabahu juu ya msingi

"wakaunganisha madhabahu juu ya nguzo" au "wakaweka madhabahu juu ya nguzo ili ibaki pale"

hofu waliokuwa nayo

huu ni msemo. AT"walikuwa na woga sana"

kwa sababu ya watu wa nchi

Unapaswa kufanya uchunguzi kitu gani kiliwahusu watu wa nchi ambacho kiliwafanya wayahudi kuogopa. AT: "kwa sababu walifikiri watu nchi walitaka kuwavamia wao"

walitoa sadaka ya kuteketezwa kwa yahwe asubuhi na jioni

kitu cha kwanza walichokifanya watu ni kuanza kutoa sadaka ya kujitoa. Hii ilikuwa kabla ya Hekalu kujengwa.

siku kuu ya vibanda

Hii ilikuwa ni sherehe ambayo ilisheherekewa kwa siku nane katika kipindi cha mwezi wa saba wa kalenda ya kiebrania. ilikuwa ikihusiana na kipindi cha kutika wakati Waisraeli wakiiishi katika mahema.

Ezra 3:6

siku ya kwanza ya mwezi wa saba

Huu ni mwezi wa saba kwa kalenda ya Kiebrania. Siku ya kwanza ilikaribia katikati ya mwezi wa tisa kwa kalenda ya watu wa magharibi.

hekalu lilikuwa bado halijapatikana

Wayahudi walianza kusherehekea kwa ibada hata kabla hawajaanza kujenga hekalu. AT:"walikuwa bado hawajaanza msingi kwa ajili ya hekalu"

kama walivyoamriwa wao kwa Koreshi mfalme wa Uajemi

Barua ilitumwa na Koreshi kuwapa wayahudi ruhusa ya kununua vifaa na kujenga hekalu.

Ezra 3:8

mwezi wa pili

Huu ni mwezi wa pili kwa kalenda ya Kiebrania. Hiki ni kipindi cha kiangazi wakati watu wanavuna mazao. Ni kipindi cha mwisho mwezi wa nne na sehemu ya kwanza kwa mwezi wa tano kwa kalenda ya magharibi.

mwaka wa pili

Hii ilikuwa ni kipindi cha mwaka ambacho baadae walirudi

kwa nyumba ya Mungu

Unapaswa kufanya uchunguzi kwamba kulikuwa hakuna nyumba ya mungu iliyokuwepo wakati wanafika.AT:"ni wapi nyumba ya Mungu ilisimamishwa" au "ni wapi walipotaka kujenga nyumba ya Mungu"

Yeshua...Yosadaki...Henadadi

Haya ni majina ya wanaume

miaka ishirini

"20 miaka"

Kadmiel

Hili ni jina la mtu. Tafsiri kama katika 2:40

Ezra 3:10

kuweka msingi

"msingi" kwa mantiki hiyo ilikuwa zaidi si matofali ya mawe kwa ajili ya kusaidia ukuta wa hekalu. Ilijumuisha sakafu yote ya hekalu iliwekewa mawe. Hii iliwawezesha wanaosifu hekaluni kuvaa mavazi lasmi na yaliwaweka kuwasafi.

nguo zao

"mavazi yao maaalum"

mkono wa Daudi... uliagiza

Mkono wa mfalme ni picha ya kumpa nguvu kutoa amri. AT:"kama Daudi alivyoagiza"

Shukrani

Hisia na kujisikia kupongeza kwa ajili ya ukarimu wa mwingine.

Ezra 3:12

nyumba ya kwanza

Hii inarejea hekalu la kwanza ambalo Selemani alijenga, nyumba ya Mungu.

mbele ya macho yao

Macho yanawakilisha kuona.AT:"katika kuona kwao" au "na walitazama"

kulia kwa sauti

Hii inaonyesha hisia ya uzuni ikiambatana na machozi na sauti ya kulia.

Ezra 4

Ezra 4:1

Taarifa kwa ujumla

Watu wasio wayahudi kujitoa kusaidia kujenga hekalu

wale waliokuwa kifungoni

Hii inaweza kutafsiriwa katika mfumo hai. AT:"wale ambao wababeli waliwachukua kifungoni"

Esar-hadoni,mfalme wa Ashuru

Alitawala Ashuru kabla ya Koreshi kutawala katika Uajemi

Zerubabeli

Jina la mtu. Tafsiri kama katika 2:1

Esar-hadoni, mfalme wa Ashuru

Alitawala katika Ashuru kabla ya Koreshi kutawala Uajemi.

Ezra 4:3

Yoshua

Jina la mtu. Tafsiri kama katika 2:3

Sio wewe, lakini sisindio lazima tujenge

Maana yake inaweza kuwa 1)viongozi wa kiyahudi walifikiri kwamba Koreshi aliwaamuru wao peke yao kujenga hekalu au 2) ujenzi wa hekalu ilikuwa ni kazi iliyowatenga wayahudi na wasio wayahudi ndio watakaoruhusiwa kuchanga kwa ajili ya kazi.

Ezra 4:4

watu katika nchi

"watu ambao walikuwa wakiishi katika nchi wakati ule" ambao ilihusisha wasio wayahudi na wayahundi ambao jamii haikuchukuliwa na Wababeli kifungoni

wakaifanya mikono ya wayahudi kudhoofika

wakawavunja nguvu wayahudi

Wayahudi

watu waliorudi kutoka Babeli na wakaweka makazi katika nchi ya Yuda

kuvuruga mipango yao

"ili kutimiza hilo wayahudi hawakujenga hekalu kama walivyokuwa wamepanga.

waliandika mashitaka dhidi ya wenyeji wa Yuda na Yerusalem

jina "mashitaka" inaweza kutafsiriwa kama kitenzi "kushitaki" na kitendo "kuishi ndani" kuheshimika. Inakupasa kufanya uchunguzi kitu gani ambacho maadui waliwashitaki wayahudi kwa walichokifanya. AT: "waliandika barua ambayo waliwashitaki wale walioishi Yudana Yerusalem kwa kutomtii mfalme"

Ezra 4:7

Bishlamu.....Mithredathi...Tabeeli.....Shimshai

majina ya wanaume

Barua

Hii ni barua iliyoongelewa katika $:4

Kiaramu

lugha iliyokuwa inatumika katika eneo hilo kwa wakati ule maalum kwa biashara

na kutafsiriwa

katika Uajemi

Rehumu

jina la mwanaume tafsiriwa kama katika

Ezra 4:9

Waelemi.....Asur

majina ya miji

Elamu

jina la mji mkubwa katika nchi

Asurbanipal

Hili ni jina la mtu

Jimbo ngambo ya mto

Hili ni jina la mji ambao ulikuwa magharibi mwa mto Flati

Ezra 4:11

Hii ni nakala

Ezra alijumuisha katika maandishi yake ujumbe wa barua kutuma kwa mfalme Artashasta

mji ngambo ya mto

Hili ni jina la mji ambalo lilikuwa magharibi ya mto Efrati. Ilikuwa ni kuvuka mto kutoka mji wa Susa. Tafsiri kama katika 4:9

mji wa uasi

Mji ni kwa watu wanaoishi hapo. AT:"mji ambao walipanga kuishi na kuwapinga ninyi"

wamekarabati msingi

"kukamilisha msingi" au "kurekebisha msingi"

Ezra 4:13

ikiwa mji utajengwa na ukuta utakamilika

Hii inaweza kutafsiriwa katika mfumo hai. AT:"Ikiwa watajenga mji na kukamilisha ukuta"

lakini watawadhuru wafalme

Neno "kudhuru" linamaanisha kwa wayahudi kutoendelea kutoa fedha kwa wafalme.

Ezra 4:14

tumekula chumvi ya Ikulu

Maana inayowezekana ni kwamab 1)mwandishi kuwa mtiifu kwa mfalme au 2)mfalme kumpa mwandishi heshima maalum. AT:"sisi ni watiifu kwako" au "umetuheshimu sisi kwa kutufanya kuwa maofisa wako"

mji wa uhalibifu

Mji ni kwa watu ambao wanaishi ndani yake.AT:"mji wanaoishi watu waliopingana dhidi ya baba yako"

mji uliharibiwa

Hii inaweza kutafsiriwa katika mfumo hai, ambapo itakulazimu kutaka kujua nani ambaye akiharibu mji. AT:"Wababeli waliharibu mji"

ikiwa mji huu na ukuta utajengwa

Hii inaweza kutafsiriwa katika mfumo hai. AT:"Ikiwa watajenga mji na ukuta" maneno haya yameonekana katika 4:13

hakuna kitakachokua kimebakia kwa ajili yako

Hii ni kumchanganya na kumfanya mfalme kufikiri kwamba hatakosa fedha nyingi za kodi iwapo wayahudi watampinga.

Mji ngambo ya mto

Hili ni jina la mji ambalo lilikuwa magharibi ya mto Efrati. Ilikuwa ni kuvuka mto kutoka mji wa Susa. Tafsiri kama katika 4:

Ezra 4:17

Mji ngambo ya mto

Hili ni jina la mji ambao ulikuwa magharibi ya mto Efrati. ilikuwa kuvuka mto kutoka mji wa Susa. Tafsiri kama katika 4:9

Barua mliyonitumia imetafsiriwa na kusomwa

Hii inaweza kutafsiriwa katika mfumo hai ambapo utatakiwa kufanya utafiti nani aliyetafsiri na kusoma barua kwa mfalme. AT:"Ninaye mtumishi kutafsiri na kusoma barua ambayo ulituma kwangu"

Rehumu

jina la mtu tafsiri kama katika 2:1

Shimshai

jina la mtu. Tafsiri kama katika 4:7

Mto

mto Efrati

Ezra 4:20

Mji ngambo ya mto

Hili ni jina la mji ambalo liko magharibi ya mto efrati. Ilikuwa kuvuka mto kutoka mji wa Susa. Tafsiri kama katika 4:9

Ada na kodi walilipwa wao

hii inaweza kutafsiriwa katika mfumo hai. AT:'Watu katika Yerusalem walilipa ada na kodi kwa wale wafalme" au "Wale wafalme waliweza kukusanya ada na kodi"

kuweka agizo

"kuweka amri"

Uwe mwangalifu usipuuze hili

"Uwe mwangalifu kufanya hili"

Kwa nini kuruhusu tishio hili kuongezeka na kusababisha hasara kwa matakwa ya mfalme?

Artashasta alitumia swali kuwaambia wao kwamba anafahamu ya kuwa atapoteza kodi na heshima ikiwa mji utajengwa. AT:"Unapaswa kuhakikisha kwamba hili tishio halikuhi na kusababisha hasara zaidi kwa matakwa ya ufalme"

tishio kukua

Hatari imeongelewa kana kwamba ulikuwa mmea ambao ungekuwa na kuongezeka kwa kimo. AT:"hatari ya kuja kuwa balaa"

kusababisha hasara zaidi kwa matakwa ya ufalme

neno "matakwa ya ufalme" ni msemo kwa mfalme mwenyewe. AT:"kusababisha mabaya mengi kutokea kwa mfalme"

Ezra 4:23

Amri ya mfalme Artashasta ilisomwa

Hii inaweza kutafsiriwa katika mfumo hai. ambapo utakiwa kufanya utafiti nani alisoma amri kutoka kwa mfalme kwa maofisa. AT:"Wajumbe kutoka kwa mfalme Artashasta walisoma amri"

Rehumu

Tafsiri kama katika

Shimshai

Tafsiri kama katika

kazi ya nyumba ya Mungu ikasitishwa Yerusalem mpaka kutawala mara ya oili kwa mfalme Dario

Huu uchelewaji ulikoma takribani miaka 16

Ezra 5

Ezra 5:1

Ido...Yoshua ...Yosadaki

majina ya wanaume

Sheatieli

jina la mtu.Kama ilivyotafsiriwa

kujenga nyumba ya Mungu

Hili lilikuwa hekalu la mungu.

Ezra 5:3

Tatenai...Shethar-Bozenai

majina ya wanaume

mji ngambo ya mto

Hili ni jina la mji ambalo ilikuwa magharibi ya mto efrati. Ilikuwa ni kuvuka mto katika mji wa Susa. Angalia kama ulivyotafsiri katika 4:9

Ezra 5:6

Hii ni nakala ya barua

Ezra anahusisha ujumbe wa barua kwa mfalme Dario kuhusiana na kazi ya hekalu.

mji ngambo ya mto

Hili ni jina la mji ambalo ulikuwa magharibi ya mto efrati. Ilikuwa kuvuka mto katika mji wa Susa. Angalia kama ilivyotafsiriwa katika 4:9

Ezra 5:8

Taarifa kwa ujumla

Barua kutoka kwa Tatenai kwenda kwa mfalme ambayo imeanza katika 5:6

mbao

ubao kwa ajili ya kujengea

nani aliyewapa waraka

"nani aliyewapa ruhusa"

Ezra 5:11

Taarifa kwa ujumla

Barua kutoka kwa Tetai kwenda kwa mfalme ambaye alianza katika 5:6 inaendelea

Sisi tu watumishi wa mmoja

Maana yake inawezekana ikiwa 1)walikuwa wakiwaita wayahudi watu wa Mungu au 2) wale waliokuwa wakijibu walikuwa wakitokea kabila la Lawi na Haruni, ambao ndio walikuwa wakiwajibika hekaluni kwa kuabudu na kutoa sadaka.

ambalo lilikuwa limejengwa miaka mingi iliyopita wakati ambapo mfalme mkuuu wa Israeli alipoujenga na kukamilisha hilo.

Hii inaweza kutafsiriwa katika mfumo hai. AT:"ambapo mfalme mkuu wa Israeli aliujenga na kusambaza vifaa vyote kwa "

Ezra 5:12

Taarifa kwa ujumla

Barua kutoka kwa Tetai kwenda kwa mfalme inaendelea. Tetai anaendelea kumwambia mfalme kile ambacho wayahudi walimwambia kuanzia katika 5:11

kumchukiza Mungu wa mbinguni

"kumfanya Mungu wa mbinguni kuwa mkali kwetu sisi"

aawatia katika mikono ya mfalme Nebukadineza wa Babeli, ambaye alivunja nyumba na kuwachukua watu

Mkono ni mfano wa nguvu au kuongoza. Pia, "kuruhusu Nebukadineza mfalme wa Babeli na jeshi lake kuvunja hii nyumba na kuwachukua watu"

Ezra 5:14

Taarifa kwa ujumla

Barua kutoka kwa Tetai kwenda kwa mfalmeambayo ilianza katika 5:6 inaendelea. Tetai anaendelea kumwambia mfalme kile ambacho wayahudi walimwambia yeye mwanzoni katika 5:11

Sheshbaza

Tafsiri kama katika

Yeye akavitunza vile

Mfalme Koreshi akavirudisha vitu vya hekalu

Na nyumba ya Mungu iweze kujengwa

Hii inaweza ktafsiriwa katika mfumo hai. AT:"ninataka wayahudi wajenge nyumba ya Mungu"

Ezra 5:16

Taarifa kwa ujumla

Barua kutoka kwa Tetai kwenda kwa mfalme ambayo ilianza katika 5:6 inaendelea. Tetai inaendelea kumwambia mfalme kile ambacho wayahudi wamemwambia yeye mwanzoni katika 5:11

imeshajengwa, lakini bado haijakamilika

Hii inaweza kutafsiriwa katika mfumo hai. AT:"watu sasa wanajenga, lakini bado hajakamilisha kazi yote"

kujengwa

kujenga

Ezra 5:17

Taarifa kwa ujumla

Barua kutoka kwa Tetai kwenda kwa mfalme ambayo inaanza katika 5:6 inaendelea. Tetai amemaliza kumwambia mfalme kile ambacho wayahudi wamemwambia yeye na sasa anamwuliza mfalme kuona kwamba kile wayahudi wamemwambia yeye ni kweli.

ikiwa hukumu ya mfalme Koreshi iko pale

"ikiwa kuna kumbukumbu kule ambapo mfalme Koreshi alitoa amri"

Ezra 6

Ezra 6:1

akaamuru uchunguzi ufanyike

Neno "uchunguzi" inaweza kuelezeka pamoja na kitenzi "kuchunguza" au "kutafuta"AT:"aliamuru maofisa wake kutafuta"

aliamuru uchunguzi

Waliambiwa kuchunguza nini inaelezwa wazi.AT:aliagiza maofisa wake kuchunguza kumbukumbu" au "aliamuru maofisa kutafuta na kujua kama kuna kumbukumbu ya mfalme Koreshi inayosema wayahudi kujenga nyumba ya Mungu katika Yerusalem"

nyumba ya kumbukumbu

Hii ni nyumba ambayo mfalme alitunza kumbukumbu muhimu za kiserikali.

Akmetha

Hili ni jina la mji

chuo kilionekana

Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai.AT:"waliona chuo" au "waliona chuo ambacho kinaeleza kuhusu Dario na Yerusalem"

Ezra 6:3

Taarifa kwa ujumla

Hii inaanza na kumbukumbu Mfalme Koreshi akiamuru kwamba wayahudi wajenge hekalu la Mungu katika Yerusalem.

Katika mwaka wa kwanza wa Mfalme Koreshi

Inaweza kuelezwa wazi kwamba huu ni mwaka wa kwanza wa kutawala. AT:"Katika mwaka 1 wa kutawala Mfalme Koreshi"

Na nyumba iweze kujengwa

Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai. AT:"Na wayahudi wajenge nyumba" au "Wayahudi lazima wajenge nyumba"

upana sitini

"60 upana" unaweza kuibadilisha kwa vipimo vya kisasa" AT:mita ishirini na saba"

sehemu tatu za mawe makubwa na sehemu ya mbao

Maana inayowezekana ni 1) hii inaonyesha jinsi ya kujenga msingi. AT:"Ijengwe katika sehemu tatu za mawe makubwa ikizungukwa na sehemu za mbao" au 2) hii inaonyesha jinsi ya kujenga ukuta. AT:"Kujenga kuta zake kwa sehemu tatu zikiwa na mawe makubwa pamoja na sehemu moja inayozunguka ya miti"

Na gharama zilipwe na nyumba ya mfalme

Msemo"nyumba ya mfalme" inamaanisha mali za mfalme Koreshi katika hazina ya ikulu. Hii inaweza kuelezwa katika mfumo hai. AT: "Nitalipa fedha hizo kutoka katika mfuko wa hazina"

Ezra 6:6

Taarifa kwa ujumla

Hii inaendeleza kumbukumbu za mfalme Koreshi kuagiza wayahudi kujenga hekalu la mungu katika Yerusalem, ambayo ilianza katika 6:3.

Tetanai...Shethar Bozenai

Dario anaandika mja kwa moja kwa huyu mtu. Tafsiri majina yao kama katika 5:3

mji ngambo ya mto

Hili ni jina la mji ambao ulikuwa magharibi ya mto eflati. Ilikuwa ni kuvuka mto kutoka mji wa Susa.

Ezra 6:8

Taarifa kwa ujumla

Hii inaendeleza kumbukumbu za Mfalme Koreshi agizo kwa wayahudi kujenga hekalu la Mungu katika Yerusalem, ambapo kilianza katika 6:3

Mchango kutoka kwa mfalme ngambo ya mto utatumika katika kuwalipa hawa wanaume.

Hii inaweza kuelezwa katika mfumo hai. AT:"Kutumia mfuko kutoka kwa mfalme ngambo ya mto utalipa hawa wanaume"

Mfuko kutoka hazina ya mfalme ngambo ya mto

"Hazina ya mfalme" inaamanisha kodi wanazolipa watu kwa mfalme. AT:"Pesa ktoka kwenye kodi ambazo mfalme anakusanya kutoka kwa watu ngambo ya mto"

Chochote kinachohitajika

Hii inaweza kutafsiriwa katika mfumo hai. AT:"chochote wanachohitaji"

Ezra 6:11

Taarifa kwa ujumla

Hii inaendelea na kumbukumbu ya mfalme Koreshi agizo kwa wayahudi kujenga hekalu la Mungu katika Yerusalem, ambalo lilianza katika 6:3

nguzo lazima itolewe katika nyumba yake na awekwe juu yake. Na nyumba yake itabadilishwa kuwa katika takataka.

Hii inaweza kutafsiriwa katika mfumo hai. AT:"Niliagiza maofisa wangu kutolewa vyuma katika nyumba na iwekwe juu yake. Na baadaye itabadilishwa nyumba kuwa katika takataka"

nguzo

kipande kirefu cha mbao, kinachosaidia paa la nyumba

ambaye amenyosha mkono kubadilisha... au kuharibu

Kunyoosha mkono inamaanisha kujaribu kufanya kitu fulani. AT:"ambaye anajaribu kubadilisha... au kuharibu"anayetaka kubadili au kuharibu"

kubadilisha hili agizo

neno "agizo" linaweza kuelezwa hivi "kitu gani nilichoagiza" AT:"kubadili kitu nilichoagiza" au "kusema kwamba nimeagiza kitu kingine kabisa"

Ezra 6:13

Tatenai...Sheshthar-Bozenai

Tafsiri majina ya hawa wanaume kama ulivyofanya katika 5:3

Nyumba ikawa imekamilika

Hii inaweza kutafsiriwa katika mfumo hai. Unatakiwa kuweka maelezo nyumba ipi iliyokamilika. AT:"Walikamilisha nyumba ya Mungu" au "Walimaliza kujenga hekalu"

siku ya tatu ya mwezi wa adari

"adari" ni jina la kumi na mbili na mwezi wa mwisho katika kalenda ya kiebrania. Ni kipindi cha majira ya baridi. Siku ya tatu ni karibu ya katikati ya mwezi wa pili wa kalenda ya magharibi.

mwaka wa sita

Mfalme dario amekuwa akiongoza kwa miaka mitano, hivyo sasa katika mwaka wa sita wa kutawala kwake.

Ezra 6:16

waliobaki wa uamisho

Hawa watu wameshikwa na kupelekwa Babeli. lakini walirudi Yerusalem. AT:"baadhi ya watu waliochukuliwa mateka kwenda Babeli na waliorudi yerusalem" au "baadhi ya watu waliorudi kutoka matekani"

ngombe mia moja...kondoo mia nne

"100 ngombe...400 kondoo

kuwapa wajibu makuhani na walawi kufanya mgawanyo

jina "mgawanyo wa kazi" unaweza kuelezewa katika msemo "kugawanya kazi katika vikundi" AT: "kugawanya makuhani na walawi katika vikundi vya kazi"

mgawanyo wa kazi

"vikundi ambavyo vinafanya kazi pamoja"

Ezra 6:19

siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza

Huu ni mwezi wa kwanza wa kalenda ya Kiebrania. Siku ya kumi na nne ni karibu ya mwanzo wa mwezi wa nne kwa kalenda ya magharibi

wakajitakasa wenyewe

"wakajiweka kuwa safi wenyewe" kuwa safi inaonyesha kukubaliwa na Mungu. AT:"wakajiweka kukubalika kwa Mungu"

Ezra 6:21

wakajitenga wenyewe kutoka kwa watu wasio safi wa nchi

Kujitenga wenyewe kutoka kwa wasio safi inaonyesha kukataa kufanya vitu ambavyo mtu kutokuwa safi. AT:"Kukataa kufanya vitu ambavyo watu wa nchi wakifanya huwafanya wao kutokuwa safi"

kutokuwa safi kwa watu wa nchi

Hapa"kutokuwa safi" inawakilisha kutokukubaliwa na Mungu. AT:"vitu ambavyo watu wa nchi walivifanya na ikawafanya wasikubaliwe na Mungu"

kumchagua Yahwe

Kumtafuta Yahwe inaonyesha kuchagua kumjua, kuabudu na kumtii yeye. AT:"kuchagua kumtii Yahwe"

kubadilisha moyo wa mfalme wa Ashuru

Kubadilisha moyo wa Mfalme inaonyesha kumfanya yeye kufikiri tofauti kuhusu kazi ya hekalu. AT:"kubadilisha tabia ya mfalme wa Ashuru" au "kufanya mfalme wa Ashuru ku kutenda"

kuwatia nguvu mikono katika kazi ya nyumba yake

kuwatia nguvu mikono yao katika kazi inaonyesha kuwasaidia wao kufanya kazi.Mfalme wa Ashuru alifanya hivi kwa kuwaabia wao kufanya kazi na kutoa fedha kwa ajili hiyo.AT:"kuwasaidia wao kufanya kazi ya nyumba yake" au "kufanya iwezekane kazi ya nyumba yake"

kazi ya nyumba yake

Hii inamaanisha kujenga hekalu

Ezra 7

Ezra 7:1

Taarifa kwa ujumla

ukoo wa Ezra unaenda mpaka kwa kuhani wa kwanza Haruna

Ezra akaja kutoka Babeli

Ezra kuja juu inaweza kutafsiriwa vizuri. AT:"Ezra akaja Yerusalem kutoka Babeli"

Seraya

Tafsiri jina hili kama ulivyofanya katika 2:1

Shalumu

Tafsiri jina la mtu huyu kama ilivyofanya katika 2:40

azaria,Hilkia,...Sadoki,Ahitubu,Amaria,Azaria,Merayothi,Zerahia,Uzi,Buki,Abishua,Fineasi,eliazari

Hii orodha ni majina wanaume wote.

Ezra 7:6

Mfalme akampa kila kitu alichoomba

"Mfalme akampa Ezra chochote alichoomba kwake"

mkono wa Yahwe ulikuwa pamoja naye

"mkono" wa Yahwe unawakilisha baraka za Yahwe au kusaidia. AT:"baraka za Yahwe zilikuwa pamoja na Ezra" au "Yahwe alikuwa akimbariki Ezra"

katika mwaka wa saba wa mfalme Artashasta

Hii inarejea mwaka wa saba wa kutawala kwake. AT:"katika mwaka wa saba ambao mfalme alikuwa Artashasta"

Ezra 7:8

mwezi wa tano

Huu ni mwezi wa tano kalenda ya Kiebrania. ni kipindi cha mwisho cha mwezi wa saba na sehemu ya awali ya mwezi wa nane katika kalenda ya Magharibi

siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza

Hii ni karibu katikati ya mwezi wa tatu katika kalenda ya Magharibi

siku ya kwanza ya mwezi wa tano

Hii ni karibu ya katikati ya mwezi wa sabakatika kalenda ya magharibi

mkono mzuri wa Mungu

"mkono" inaonyesha nguvu au uongozi ambao Mungu anatumia kwa matokeo mazuri.

Ezra akaendeleza moyo wa kujisomea

Kuendeleza moyo inamaanisha kuamua au kujitoa yeye binafsi kufanya kitu fulani. AT:"ezra alijitoa maisha yake katika kusoma"

kutoa nje

"kutii"

maagizo na sheria za Yahwe

Hizi ni sheria ambazo Mungu alizileta kwa Waisrael kwa kumtumia Musa

Ezra 7:11

Hili lilikuwa agizo

ujumbe uliofuata maelezo lilikuwa agizo lililotolewa na mfalme Artashasta

Mfalme wa wafalme Artashasta

"Mfalme wa wafalme" ulikuwa ni wasifu, ukiwa unamaanisha kwamba alikuwa mkuu wa wafalme, mfalme ambaye wafalme wengine walimtii. AT:"Mfalme mkuu Artashasta" au "Artashasta, mkuu mfalme"

Ninatoa amri kwamba mtu yeyote....ambaye anatamani kwenda Yerusalem

Katika siku zile watu walipenda ruhusa kutoka kwa mfalme kurekebisha na kujenga katika eneo zamani liliharibiwa na wavamizi wa taifa jingine.

wanaweza kwenda pamoja na wewe

Neno "wewe" linamaanisha Ezra.

Ezra 7:14

Maelezo ya kuhusisha

Hii inaendelea na agizo la mfalme Artashasta alilompa ezra

Mimi, mfalme, na washauri wangu saba

neno "mimi" na msemo "Mfalme" linamaanisha mtu huyo huyo. Mfalme anakumbusha watu ambao watasikia barua kwamba yeye ndio mhusika wa hiyo barua.

kufahamu kuhusu Yuda na Yerusalem kuhusiana na sheria ya Mungu

kitu ambacho walitakiwa kuhulizia kinaweza kuelezewa vizuri zaidi. AT:"kuchunguza mwenendo katika Yuda na Yerusalem, ili kujifunza endapo au awatii sheria za Mungu"

Inakupasa kuleta dhahabu na fedha

Kitu walichoambiwa kuleta kinaweza kuelezwa vizuri.AT:"Inakupasa kuleta Yerusalem fedha na dhahabu"

fedha na dhahabu ambazo walitoa kwa hiari

"Hiari" inamaanisha hawakulazimishwa kutoa fedha. Walitoa kwa sababu walitaka. AT:"dhahabu na fedha ambazo walihiari kutoa"

Kitu gani cha hiari kilichotolewa na watu pamoja na makuhani

Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai. AT:"Kitu gani watu na makuhani walitoa kwa hiari"

Ezra 7:17

maelezo ya kuhusisha

Hii inaendelea na agizo ambalo mfalme Artashasta alimpa Ezra

Basi ununue vyote...sadaka

msemo"vyote" inamaanisha vingi na vya muhimu kumalizia kazi. Walipaswa kutumia dhahabu na fedha kununua vyote vinavyohitajika ili kumwabudu mungu katiak hekalu. AT:"Nunua vingi kondoo, beberu,unga na sadaka ya vinywaji kama inavyohitajika"

wewena ndugu zako

Msemo "ndugu zako" inamaanisha watu ambao walifanya kazi pamoja na Ezra. AT:"watumishi wenzako" au "washirika wako"

Ezra 7:19

Maelezo ya kuhusisha

hii inaendeleza agizo ambalo mfalme Artashasta alimpa Ezra.

vitu ambavyo ulipewa kwa hiari wew

Hii inaweza kutafsiriwa katika mfumo hai. AT:"Vitu ambavyo tumevitoa kwa hiari kwako"

Viweke vitu...mbele yake yeye

Neno "yeye" linamaanisha Mungu

kwa huduma ya nyumba ya Mungu wako

Neno "huduma" linaweza kuelezwa kwa kitendo "kuhudumia" au "kutumia" "kazi" au "kuabudu" AT:"kutumia katika nyumba ya Mungu wako" au :kutumika katika nyumba ya Mungu wako"

hazina

sehemu ya usalama ambapo fedha inatunzwa

Ezra 7:21

Maelezo ya kuhusisha

Hii inaendelea na agizo ambalo mfalme Artashasta alimpa Ezra

mji ngambo ya mto

Hili ni jina la mji ambao ulikuwa magharibi mwa mto Efrati. Ilikuwa ni kuvuka mto kutoka mji wa Susa. Angalia ulivyotafsiri katika 4:9

Chochote ambacho Ezra ataomba kwenu anapaswa kupewa chote

Hii inaweza kutafsiriwa katika mfumo hai. "Mpeni Ezra chote anacjooomba kwenu"

anapaswa kupewa chote

Msemo "chote" hapa inamaanisha vyovyote muhimu vya kufanyia kazi. AT:"anapaswa kupewa vingi kadri anavyohitaji"

talanta mia moja za fedha

"talanta 100 za fedha" Unaweza kuthamanisha hii kwa kiwango cha sasa. AT:"3,400 talanta za fedha" au "tani tatu na nusu"

vipimo miavya ngano

Unaweza kuthamnisha katika kipimo cha sasa. 22,000 lita za ngano" au "ishirini na mbili elfu lita za ngano"

bathi mia za mafuta

Unaweza kuzibadilisha katika kipimo cha sasa. AT:"22,000 lita za mafuta" au "lita elfu mbili za mafuta"

nyumba yake

Hii inamaanisha hekalu la Mungu

Kwa nini hasira yake ije kwenye ufalme wangu na watoto wangu?

Mfalme anatumia swali hili kusema kwamba hataki hasira ya mungu ifike kwao. Hii inaonyesha kwamba wasipompa ezra kile ambacho ametaka, ndipo Mungu ataupiga ufalme. AT:"Kwa kuwa hatutaki hasira ya Mungu ije kwetu katika ufalme wangu na watoto" au "kwa kuwa usipofanya vitu hivi , hasira ya Mungu itakuja juu ya ufalme wako na watoto wako"

Kwa nini hasira yake ije ufalme wangu na watoto wangu

Hasira ya Mungu inamaanisha Mungu kuwaadhibu wao.AT:"Kwa nini Mungu kuadhibu ufalme wangu na watoto" au :Kwa kuwa usipofanya vitu hivi, Mungu ataadhibu ufalme wangu na watoto"

Ezra 7:24

Maelezo ya kuhusisha

Hii inaendelea kuhusisha agizo ambalo mfalme Artashasta alimpa Ezra.

Tutawapa taarifa wao kuhusu ninyi kwamba wasiwatoze ushuru au kodi

"Tumewaambia wao wasiwatoze ushuru au kodi"

mwanamuziki

watu wanaopiga vifaa vya muziki

Ezra 7:25

Maelezo ya kuhusisha

Huu ni mwisho wa agizo la mfalme Artashasta alimpa Ezra

kwa hekima aliyokupa Mungu, inakulazimu kuteua waamuzi na mtu muelewa

Jina "hekima" inaweza kuelezwa kwa neno "busara" na "hekima" AT:"Mungu amekupa hekima, hivyo hekima utateua waamuzi na mtu muelewa"

ikiwezekana kwa kifo, kuhamishwa, kuchukuliwa mali zake au kufungwa.

jina linaweza kutafsiriwa kama kitendo. AT:"uenda kwa kuwaua wao,kuwahamisha,kutowesha vitu vyao, au kuwafunga wao" "unaweza kuwaua wao, kuwafukuza wao, kuchukua vitu wanavyomiliki au kuwaweka gerezani"

Ezra 7:27

Maelezo ya kuhusisha

Ezra anamtukuza Mungu kwa sababu ya agizo la mfalme Artashasta

aliweka ndani ya moyo wa mfalme ili kumtukuza nyumba ya Yahwe katika Yerusalem

kuweka vitu ndani ya moyo wa mfalme inamaaanisha kusababisha yeye kuwa mawazo na matakwa. AT:"kusababisha mfalme kutaka kumtukuza nyumba ya Yahwe katika Yerusalem

Nyumba ya Yahwe

Hii inamaanisha hekalu la Yahwe

Nilitiwa nguvu

kutiwa nguvu inamaanisha kutiwa moyo. AT"Nimetiwa moyo"

kwa mkono wa Yahwe Mungu wangu

Hapa mkono wa Mungu inamaanisha alichokifanya kumsaidia Ezra. AT:"kwa sababu Yahwe amenisaidia mimi"

Ezra 8

Ezra 8:1

Taarifa kwa ujumla

Kuna badiliko la umiliki kuanzia hapa. Sura ya 1 - 7 iliandikwa kana kwamba mhusika alikuwa akiandika kuhusu Ezra. Sura ya 8 iliandikwa kana kwamba mhusika ni Ezra

Taarifa kwa ujumla

Mstari 2 - 14 ni orodha ya viongozi na watangulizi wao. Wote walikuwa ni wanaume

mwana wa Finehasi, Gershoni

Hii ni kitu cha kwanza katika orodha. Inaweza kuandikwa pamoja na kitenzi "ilikuwa" AT:"Kiongozi wa wana wa Finehasi alikuwa Gershoni" au "Gershoni alikuwa kiongozi wa wana wa Finehasi"

wana wa Ithamari,Daniel

Hiki ni kitu cha pili katika orodha. Kinaweza kuandikwa kwa kitendo "ilikuwa" AT:"Kiongozi wa wana wa Ithamari alikuwa Daniel" au "Daniel alikuwa kiongozi wa wana wa Ithamari"

Paroshi

Tafsiri jina la huyu mtu kama ulivyofanya katika 2:3

mwana wa Daudi, ambao walikuwa... Paroshi na Zakaria

Hii ni kitu cha tatu katika orodha. inaweza kuandikwa kama kitendo "walikuwa" AT:"Viongozi wa wana wa Daudi walikuwa Hatishu ambaye alikuwa Paroshi na Zakaria" au "Kiongozi wa wana wa Daudi walikuwa Hatishu na Zakaria. Hatishu alikuwa kutoka ...Paroshi"

pamoja na yeye walikuwa 150 wanaume waliorodheshwa katika kumbukumbu ya ukoo.

"pamoja na Zakaria walikuwa 150 wanaume waliorodheshwa katika kumbukumbu ya ukoo"

Ezra 8:4

Taarifa kwa ujumla

Orodha ya majina ya wanaume yanaendelea

wana wa Pahath-Moab,Eliehoenai mwana wa Zerahia

"Elihoenai mwana wa Zerahia alikuwa kiongozi wa wana wa Pahath Moab"

na pamoja naye kulikuwa wanaume mia mbili

"na pamoja Eliehoenai kulikuwa wanaume mia mbili"

Zerahia

Tafsiri jina la mtu huyu kama ulivyofanya katika 7:1

Shekania

Tafsiri jina la mtu huyu kama ulivyofanya katika 8:1

adini

Tafsiri jina hili kama ulivyofanya katika2:15

mia mbili...mia tatu...hamsini...sabini

"200...300...50...70"

Ezra 8:8

Taarifa kwa ujumla

Orodha ya majina ya wanaume inaendelea

wana wa Shephatia,Zebadia mwana wa Mikaeli

Hiki ni kitu cha pili katika orodha. Kinaweza kuandikwa pamoja na kitendo "ilikuwa." AT:"Kiongozi wa wana wa Shephatia alikuwa Zebadia mwana wa Mikaeli" au "Zebadia mwana wa Mikaeli alikuwa ni kiongozi wa wana wa Shephatia"

Shephatia

Tafsiri jina la mtu huyu kama ulivyofanya katika 2:3

Mikaeli

Hili ni jina la mtu.

na pamoja naye walikuwa wameorodheshwa wanaume themanini

"na pamoja na Zebadia walikuwa wameorodheshwa wanaume themanini"

Bebai

Tafsiri hii kama ulivyofanya katika 2:11

themanini...ishirini...nane

nane- "80...28"

Ezra 8:12

Taarifa kwa ujumla

Huu ni mwisho wa orodha ya majina ya wanaume

wana wa Azgadi,Yohana mwana wa Hakatani

Hii ni kitu kinachofuata katika orodha. Inaweza kuandikwa pamoja na kitenzi "ilikuwa" AT:"Kiongozi wa wana wa Azgadi alikuwa Yohana mwana wa Hakatani" au "Yohana mwana wa Hakkatani alikuwa kiongozi wa wana wa Azgadi"

na pamoja naye walikuwa wameorodheshwa wanaume 110

"na pamoja na Yohana waliorodheshwa wanaume 110"

Wale wa wana wa adinikamu

Neno "wale" linamaanisha viongozi. AT:"Viongozi wa wana wa Adonikamu"

AZgadi

Tafsiri jina hili la mtu kama ulivyofanya katika 2:11

Adonikamu

Tafsiri jina hili la mtu kama ulivyofanya katika 2:11

Bigvai

Tafsiri jina la mtu huyu kama ulivyofanya katika 2:1

sitini...sabini

"60...70"

Ezra 8:15

Taarifa kwa ujumla

Neno "mimi" katika sura 8 linamaanisha Ezra. Yeye ni mhusika.

Taarifa kwa ujumla

Mstari 16 unajumuisha orodha ya majina ya wanaume

mto uliyokuwa unaelekea Ahava

Maana inaweza kuwa kwamba "bandari" ilkuwa 1)njia ya maji ambayo watu walitengeneza au 2) mto wa kawaida. Inaweza kutafsiriwa kwa njia moja ya ujumla. AT:"njia ya maji ambayo inaelekea Ahava"

Ahava

Hili ni jina la eneo

Shemaya

Tafssiri jina la mtu huyu kama ulivyofanya katika 8:12

Elnathani...Elnathani...Elnathani

Kulikuwa na uwezekano wanaume watatu pamoja waliofanana majina.

Ezra 8:17

Ido

hili ni jina la mtu

Kilichofuata niliwatuma wao kwa Ido

Neno "wao" linamaanisha viongozi tisa na walimu wawili walioandikwa katika 8:15. AT:"kilichofuata niliwatuma wale wanaume kwa Ido"

Kasifia

Hili ni jina la eneo

niliwaambia wao chakusema kwa Ido..kwamba , kutumakwetu watumishi kwa ajili ya nyumba ya Mungu

Neno "kwamba" linaonyesha kuwa aliwaambia wao kusema. AT:"Niliwaambia wao kumwambia Ido...kutuma kwetu watumishi kwa ajili ya nyumba ya Mungu"

Ezra 8:18

sherebiah...Mali...Hashabiah...Yeshaya...Merari

Haya ni majina ya wanaume

Hivyo wakatutuma sisi kwa Mungu na mkono mzuri wa mtu

Mungu "mkono mzuri" unawakilisha ukarimu wake katika kuwapatia wao. AT:"Kwa sababu Mungu alikuwa mwema kwetu,walituma kwetu mtu"

mtu makini

huyu ni mtu mwenye ufahamu na hekima.

mwana wa Levi mtoto wa Israeli

Hapa "Israel" ni jina la mtu. Ni jina ambalo Mungu alimpa Yakobo.

kumi na nane...ishirini

18,20.

Yeshaya

Tafsiri jina hili kama ukatika 8:4

maofisa

watu ambao wana mamlaka maalum katika muundo wa Serikali

Ezra 8:21

mto wa Ahava

Hili ni jina la bandari ambayo elekeza maji eneo linaloitwa Ahava. Angalia ulivyotafsiri Ahava na bandari katika 8:15.

kutafuta njia ilinyooka kutoka kwakwe kwa ajili yetu,watoto wadogo na mali zetu zote

Neno "kutafuta" inamaanisha kumwomba Mungu afanye kitu kwa ajili yao. Hapa "njia iliyonyooka" inawakilisha usalama wakati wanasafiri. AT:"tunapomwomba Mungu kutupa sisi, wadogo zetu, na mali zetu usalama wakati wa safari" au "Kumwomba Mungu kutulinda sisi, wadogo zetu na mali zetu zote wakati tunasafiri"

Mkono wa Mungu wetu uko pamoja na wale wanaomtafuta

mkono wa Mungu unapokuwa pamoja na watu ni msemo kuwa Mungu husaidia watu. Kumtafuta Mungu ni msemo kuwa kumtumikia yeye" AT:"Mungu husaidi wote a,bao wanamtumikia yeye"

lakini uweza wake na ghazabu yake ni juu ya wale wote wanaomwasi yeye

Uwezo wa Mungu na gjazabu kuwa juu ya watu ni msemo kwake kuwa atawaadhibu watu. kumsahau Mungu ni msemo kwamba kukataa kumtumikia yeye. AT:"lakini yeye hutoa adhabu kwa wote ambao wanakataa kumtumikia yeye"

Hivyo tulifunga na kumsihi Mungu kwa jambo hili

Hapa kumtafuta mungu ni msemo wa kumwomba mungu afanye kitu kwa ajili yao. AT:"Hivyo tulifunga na kumwomba Mungu atusaidie sisi"

Ezra 8:24

Sherabia,Hashabia

Tafsiri majina haya ya wanaume kama ulivyofanya katika 8:18

Ezra 8:26

650 talanta za fedha

"650 talanta za fedha," Unaweza kuibadilisha hii katika kipimo cha sasa. AT:"22,000 kilogram za fedha" au "ishirini na mbili elfu kilogram za fedha"

talanta mia moja za vyombo vya fedha

Unaweza kubadilisha hii katika kipimo cha sasa. AT:"3,400 kilogram vyombo vya fedha"

talanta mia moja za dhahabu

Unaweza kuibadili hii katika kipimo cha sasa. AT:"3,400 kilogram ya dhahabu"

elfu moja darkoni

"darkoni"ilikuwa ni salafu ndogo ya dhahabu ambayo watu wa utawala uajemi waliitumia. Unaweza kutafsiri kwa idadi ya salafu au kwa uzito wake. AT:"Salafu elfu moja za dhahabu ya Uajemi au "kilogram nane na nusu za dhahabu"

vyombo vilivonakshiwa

Vyombo vilivyonakshiwa ni mchanganyiko wa shaba na chuma. Ina uimara zaidi ya shaba

Ezra 8:28

Ndipo nikasema kwao

"Ndipo nikawaambia maofisa kumi na mbili wa kikuhani"

ndipo mtakapovipima mbele ya makuhani,walawi na viongozi

Walipofika Yerusalem , walipima fedha, dhahabu na vyombo ili kuonyesha kwamba hawakuchukua chochote kwa ajili yao binafsi.

Makuhani na Walawi

Kulingana na sheria ya Musa, kabila la Levi walikuwa na kazi ya kutunza hekalu, mali zake pamoja na sadaka.

Ezra 8:31

Tukatoka kwenda mto Ahava

"Tuliuacha mto Ahava" au "Tulianza kusafiri kutoka mto Ahava"

Mto Ahava

hili ni jina la mto ambao unaosafiri kwenda sehemu inayoitwa ahava. Tafsiri hii kama ulivyofanya katika 8:21

siku ya kumi na mbili ya mwezi wa kwanza

Hii ni mwezi wa kwanza wa kalenda ya kiebrania. Siku ya kumi na mbili ya karibu ya mwisho wa mwezi wa tatu kalenda ya magharibi.

Mkono wa Mungu ulikuwa juu yetu

Mkono wa Mungu kuwa juu ya watu ni msemo wa Mungu kusaidia watu. AT:"Mungu alikuwa akitusaidia sisi"

alitulinda kutoka kwenye mikono ya adui na wale...njiani

Mkono unawakilisha kile ambacho watu wangefanya. Inawalenga wao kuvamia kikundi ambacho walikuwa wanasafiri. AT:"alitulinda sisi kutokana na uvamizi wa adui na wale ambao walitaka kutuzuru tukiwa njiani" au " Aliwazuia maadui kutuvamia sisi na aliwazuia wanyanganyi kutotuzuru sisi tukiwa njiani"

wale waliotaka kutunfanyia fujo sisi

Hii inamaanisha wezi na wanyanganyi ambao walitaka kuwavamia wao kwa kuchukua fedha.

Ezra 8:33

fedha,dhahabu na vyombo vilipimmwa nje

Hii inweza kutafsiriwa katika mfumo hai. AT:"maofisa kumi na wawili wa kikuhani walipima fedha,dhahabu na vyombo.

waliweza kupima nje...kwamkono wa Meremothi

waliweza kupima nje..kwa mkono wa meremothi

Meremothi...Uriah...Eleazari...Phineasi...Yozabadi...Yoshuhua....Noadia..Binui

Haya ni majina ya wanaume

Yoshua

Tafsiri jina la mtu huyu kama ulivyofanya katika 2:3

Ezra 8:35

Wale waliorudi kutoka mateka...watu wa kifungoni

Hii misemo miwili inamaanisha wayahudi ambao walikuwa wakiishi Babeli utumwani na ambao walitoka Babeli na kurudi Yerusalem katika Yuda. AT:"wale waliorudi Yerusale kutoka kifungoni Babeli, watu wa matekani"

kumi na mbili...tisini...sita...sabini na saba...kumi na mbili

sita...sabini-saba...kumi na mbili "12...96...77...12"

maofisa katika mji ngambo ya mto

Hawa walikuwa ni maofisa wa Babeli waliokuwa wakiongoza watu magharibi ya mto Efrati, pamoja na watu walioishi Yuda.

mji ngambo ya mto

hili ni jina la mji ambao ulikuwa magharibi ya mto Efrati. Ilikuwa ni kuvuka mto kutoka mji wa Susa. Ilijumuisha Yuda. angalia ulivyotafsiri katika 4:9

Nyumba ya Mungu

hekalu

Ezra 9

Ezra 9:1

hawakuweza kujitenga wenyewe

wameoana na watu kutoka nchi nyingine na wamefuata dini zao

Ezra 9:3

Niliposikia haya

Ezra aliposikia kwamba Waisraeli wengi wameoa wanawake wa kigeni na walikuwa wakiabudu miungu yao

nikachana nguo zangu na kanzu yangu na kunyoa nwele kichwani na ndevu

Ezra alikuwa akionyesha kila mmoja jinsi asivyopendezwa na watu walivyofanya mamboyaliyomchukiza Mungu

sadaka za jioni

sadaka ambayo makuhani wangeitoa kipindi ambacho jua linazama

Ezra 9:5

nafasi yangu nikiwa mnyenyekevu

njia nyingine ya kusema yeye alikuwa "alikaa na aibu"(9:3). "nilipokuwa nimekaa kwenye kiwanja chini kuonyesha aibu niliyokuwa nayo"

nikapiga na kunyooosha mikono yangu

"nikatoka na magoti yangu na kujinyoosha viungo nikiwa nimenyoosha mikono kuelekea angani

makosa yetu yamekuwa hadi kuvuka kichwani na maovu yetu yameongezeka kufika mbinguni

Haya maneno yana jinsi mbili ya kuyaongea makosa na maovu kana kwamba ni mwili abao unaweza kukuwa na kuongezeka kama watu. Majina "makosa" na "maovu" yanaweza kuelezekeza kama jina na kivumishi. AT:"sisi tumetenda maovu na tuna makosa"

Ezra 9:7

siku za watangulizi wetu

"wakati ambapo watangulizi wetu walikuwa hai"

katika maovu makuu...katika makosa yetu

Neno "maovu" na "makosa" yanaweza kutafsiriwa kama kitenzi na kitendo, respectively. AT:"maovukweli...Kwa sababu ya uovu tulioufanya:

sisi...tulikabidhiwa kwenye mikono ya mfalme

Hii inaweza kutafsiriwa kwenye mfumo hai.AT:ulitupa sisi...kwenye mikono ya mfalme"

kwa upanga

Upanga ni msemo wa watu kuua watu wengine. Mungu aliruhusu watu kuwaua wayahudi.

matekani

Hili jina linaweza kutafsiriwa kama kitendo. Mungu aliruhusu watu kuwakamata wayahudi na kuwachukua na kuwapeleka.

Ezra 9:8

neema kutoka kwa Yahwe Mungu wetu imekuja

Mungu ameamua kuonyesha rehema imesemwa kwetu ikiwa neema angekuwa mtu ambaye anaweza kutembea. AT:"Yahwe Mungu wetu ameamua kuwa mwenyerehema kwetu na"

ameendeleza agano kwa uaminifu kwa ajili yetu

Agano la uaminifu limesemwa kana kwamba ni kitu ambacho mtu anaweza kukishirikilia mkononi mwake na kukigawa kwa mtu mwingine kukichukua. AT:"alitoa ili iwe uaminifu kwetu sisi na kutunza Agano lake"

mbele ya macho kwa mfalme wa Uajemi

Kiualisia mfalme asingeweza kuona hekalu, lakini alijua kuhusu kilichokuwa kinatokea katika Yerusalem. Hapa "macho" ni msemo kwa kile ambacho mtu anafahamu. AT:"Hivyo mfalme wa Uajemi alijua kuhusu hilo"

Nyumba ya Mungu

hekalu

atatupatia sisi msingi salama

Msingi ambao utawaweka watu salama ni fumbo kwa Yahwe atawalinda watu wake. AT:"atatulinda sisi salama"

Ezra 9:10

kwa wakati wote

"mpaka mwisho wa wakati"

Ezra 9:13

matendo yetu maovu na makosa yetu makuu

najina :maovu" na "makosa" yanaweza kutafsiriwa kama majina na kivumishi. AT:"kwa sababu ya mambo mabaya tuliyofanya na kwa sababu tulikuwa na makosa"

hukutazama makosa yetu na kutuadhibu tulivyostahili na kutuacha kama mabaki

"ulikuwa na haki kama ungetuangamiza sote, lakini ukutuadhibu na matokeo yake ukatuacha tukiwa hai"

tunaweza kuvunja tena amri zako na kufanya...watu?

Hii inaweza kutafsiriwa kama maelezo.AT: "hili ni kosa kubwa sana kwamba baadhi tumevunja amri zako na kufanya ...watu."

huwezi kuwa na hasira....kutoroka?

Hii inaweza kutafsiriwa kama maelezo.AT:"ninaogopa kwamba utachukia....kutoroka"

Ezra 9:15

Angalia

"Kuwa makini kwa kile ambacho nataka kusema"

Tuko mbele yako na makosa yetu

"Utaona kwamba sisi sote tuna makosa"

hakuna hata mmoja anayeweza kusimama mbele yako

"hufikiri kwamba mtu yeyote ana kosa"

Ezra 10

Ezra 10:1

Akiwa Ezra anaomba na kutubu...akajirusha mwenyewe chini

Ezra anajiongelea mwenyewe kana kwamba alikuwa mtu mwingine

akajirusha mwenyewe chini

upesi kutoka katika hali ya kusimama na kuwa hali ya kulala uso ukiangalia chini

mbele ya nyumba ya Mungu

mbele ya hekalu

Shekania

Kama ilivyotafsiriwa katika 8:4

Yehieli

Kama ilivyotafsiriwa katika 8:8

Tumekuwa sio waaminifu kwa Mungu wetu

Hii ilifanywa kama toba ya hadharani, sio madai ya kujivuna

Ezra 10:3

Sisi tuko pamoja nawe

"sisi tutakusaidia wewe"

Ezra 10:5

Yehohanani...Eliashibu

Haya ni majina ya wanaume

Ezra 10:7

Yeyote ambaye hakuja...atachukuliwa mali zote na kutengwa

"<aofisa watachukua mali yote kutoka mtu yeyote asiyekuja... na watawatenga wao" au "Watu wa Yuda na Yerusalem watachukua mali yote kutoka kwa yeyote ambaye hakuja ... na watawatenga wao"

siku tatu

3 siku

Ezra 10:9

katika siku tatu

"siku tatu baadaye"

mwezi wa tisa na siku ya ishirini ya mwezi

Huu ni mwezi wa tisa wa kalenda ya kiebrania. Siku ya ishirini ni karibu katikati ya mwezi wa kumi na mbili kwa kalenda ya watu wa magharibi.

katika mraba

sehemu kubwa ya uwazi mbele ya hekalu

Walijitoa kutetea

jina "kujitetea" linaweza kutafsiriwa kama kitenzi. AT: "kusaidia adui za watu wako"

na kama kuongeza makosa ya Waisraeli

'na sasa Mungu akatuona wenye makosa zaidi ya dhambi kuliko mwanzoni"

Ezra 10:11

mjitenge kutoka

kuondoka kutoka, kuwa tofauti kutokana

Ezra 10:12

hii sio siku moja au mbili za kazi

Hii inaweza kutafsiriwa katika mfumo chanya. AT: Tutahitaji muda mrefu kufanya hii kazi yote"

Ezra 10:14

muda uliopangwa na viongozi wa mji na waamuzi wa mji

Hii inaweza kutafsiriwa katika mfumo hai. AT:"muda ambao viongozi na waamuzi wa mji wataupanga"

Yonathani...Asaheli...Yazeya...Tikwa...Meshulamu.......Sh

majina ya wanaume

Yonathani mwana wa Asaheli na Yazeya mwana wa Tikwa wakapinga hili

Maana inaweza kuwa 1) hawa watu hawakutaka wakuu wa mji kuchunguze maovu au 2) hawakutaka mtu yeyote kuchunguza ndoa za watu.

Ezra 10:16

walifanya hivi

watu walichunguza wale ambao walioa wasio wayahudi

siku ya kwanza ya mwezi wa kumi

Huu ni mwezi wa kumi wa kalenda ya Kiebrania. Siku ya kwanza inakaribia katikati ya mwezi wa kumi na mbili kwa kalenda ya watu wa magharibi.

siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza

Hii ni katikati ya mwezi wa tatu kwa kalenda ya magharibi

Ezra 10:18

Yoshua

Kama ilvyotafsiriwa katika 2:1

Yosadaki

Kama ilivyotafsiriwa katika 3:1

Maasela...Gedaliah

majina ya wanaume

Eliazeri...Yaribu

Kama ilivyotafsiriwa katika 8:15

Ezra 10:20

Taarifa kwa ujumla

Ezra anaendelea kuorodhesha wanaume ambao walioa wanawake wasio wayahudi

Imeri...Pashuri

majina ya wanaume

Hanani...Elionai...Nethanai...Elasa

majina ya wanaume

Zebadia

jina la mtu. Kama ilivyotafsiriwa katika 8:8

Harimu

jina la mtu, Kama ilivyotafsiriwa katika 2:31

Maaseya

jina la mtu. kama ilivyotafsiriwa katika 10:18

Shemaya...Yehieli

majina ya wanaume.Kama iilivyotafsiriwa katika 8:12

Yozabadi

jina la mtu. Kama iivyotafsiriwa katika 8:33

Ezra 10:23

Taarifa kwa ujumla

Ezra anaendelea kuorodhesha wanaume ambao walioa wanawake wasio wayahudi

Yozabadi

jina la mtu. Kama ilivyotafsiriwa katika 8:33

Eliashibu

jina la mtu. Kama ilivyotafsiriwa katika 10:5

Shalumu

jina la mtu. kama ilivyotafsiriwa katika 2:40

Paroshi

jina la mtu. Kama ilivyotafsiriwa katika 2:3

Eliazari

jina la mtu. Kama ilivyotafsiriwa katika 7:1

Ezra 10:26

Taarifa kwa ujumla

Ezra anaendle akuorodhesha wanaume ambao walioa wanawake wasio wayahudi

Elamu...Zatu...Bani

Majina ya wanaume.Kama ilivyotafsiriwa katika 2:7

Yehieli

jina la mtu. Kama ilivyotafsiriwa katika 8:8

Elionai

jina la mtu. Kama ilivyotafsiriwa katika 10:20

Eliashibu...Yehohanani

majina ya wanaume. Kama ilivyotafsiriwa katika 10:5

Bebai

jina la mtu. kama ilivyotafsiriwa katika 2:11

Yehohanani

jina la mtu. kam ilivyotafsiriwa katika 10:5

Meshulamu

jina la mtu. Kam ilivyotafsiriwa katika 8:15

Ezra 10:30

Taarifa kwa ujumla

Ezra anendelea kuorodhesha wanaume ambao wameoa wanawake wasio wayahudi

Pahathi Moabu

jina la mtu. Lama ilivyotafsiriwa katika 8:4

Benaya...Matania

Majina ya wanaume. kama ilivyotafsiriwa katika 10:23

Maaseya

jina la mtu. Kama ilvyotafsiriwa katika 10:18

Mattania

jina la mtu. Kama ilivyotafsiriwa katika 10:26

Binui

jina la mtu. kama ilivyotafsiriwa katika 8:33

Harimu

jina la mtu. kama ilivyotafsiriwa katika 2:31

Eliezeri

jina la mtu. Kama ilivyotafsiriwa katika 8:15

Maluki

jina la mtu. Kama ilivyotafsiriwa katika 10:26

Ezra 10:33

Taarifa kwa ujumla

Ezra anaendelea kuorodhesha wanaume ambao walioa wanawake wasio wayahudi

Hashumu

jina la mtu. kama ilivyotafsiriwa katika 2L19

Zabadi

jina la mtu. Kama ilivyotafsiriwa katika 10:26

Elifereti

jina la mtu. kama ilivyotafsiriwa katika 8:12

Manase

jina la mtu. kama ilivyotafsiriwa katika 10:30

Shimei...Benaya

majina ya wanaume. Kama ilivyotafsiriwa katika 10:23

Bani

jina la mtu. Kama ilivyotafsiriwa katika 2:7

Meremothi

jina la mtu. Kama ilivyotafsiriwa katika 8:33

Eliashibu

jina la mtu. kama ilivyotafsiriwa katika 10:5

Ezra 10:37

Taarifa kwa ujumla

Ezra anaendelea kuorodhesha wanaume ambao walioa wanawake wasio wayahudi

Matania...Adaya

majina ya wanaume.Kama ilivyotafsiriwa katika 10:26

Matenai

jina la mtu. Kama lilivyotafsiriwa katika 10:33

Binui

jina la mtu. Kama lilivyotafsiriwa katika 8:33

Sheremiah

jina la mtu. Kama lilivyotafsiriwa katika 10:23

Ezra 10:41

Taarifa kwa ujumla

Ezra anamaliza kuorodhesha wanaume ambao walioa wanawake wasio wayahudi

Sheremia

jina la mtu. kama lilivyotafsiriwa katika 10:37

Shalumu

jina la mtu. Kama lilivyotafsiriwa katika 2:40

Amaria

Jina la mtu. Kama lilivyotafsiriwa katika 7:1

Nebo

jina la mtu. Kama lilivyotafsiriwa katika 2:27

Yeieli

jina la mtu. Kama lilivyotafsiriwa katika 8:12

Zabadi

jina la mtu. Kama lilivyotafsiriwa katika 10:26

Ido

jina la mtu. Kama lilivyotafsiriwa katika 5:1

Benaya

jina la mtu. Kama lilivyotafsiriwa katika 10L23

Hawa wote

wanaume wote katika orodha kuanzia katika 10:20

Nehemiah 1

Nehemiah 1:1

Nehemia .....Hakalia .... Hanani

Haya ni majina ya watu

katika mwezi wa Kisleu

'Kislev' ni mwezi wa tisa wa kalenda ya Kiebrania. Ni wakati wa mwisho wa Novemba na sehemu ya kwanza ya Desemba kwenye kalenda za Magharibi.

katika mwaka wa ishirini

Nehemia akimaanisha idadi ya miaka ambayo Artaxerxes alikuwa ametawala akiwa mfalme. AT 'mwaka wa ishirini wa utawala wa Artaxerxes, Mfalme wa Uajemi

mji mkuu wa Sushani

Hii ilikuwa moja ya miji ya kifalme ya wafalme wa Kiajemi, iliyo katika nchi ya Elamu. Ilikuwa jiji kubwa, yenye ngome yenye kuta za juu zilizozunguka.

mmoja wa ndugu zangu

Hanani alikuwa ndugu wa Nehemia wa kiroho.

Hanani, alikuja pamoja na watu wengine kutoka Yuda

Hanani alikuja kutoka Yuda na watu wengine'

Wayahudi waliopona, Wayahudi waliosalia waliokuwa huko

Maneno haya mawili yanataja kundi moja la watu. Maana inawezakuwa ni 1) Wayahudi wachache ambao walichukuliwa kama wahamisho Babeli lakini waliokoka na kurudi kuishi Yerusalemu au 2) Wayahudi wachache ambao waliokoka kutoka kwa wale waliokuwa wakijaribu kuwapeleka uhamishoni huko Babiloni na hivyo wakaa Yerusalemu. Kwa kuwa haijulikani wapi walipokimbia, inaweza kuwa bora si kutaja katika tafsiri. AT "Wayahudi ambao waliokoka uhamisho na waliobaki Yerusalemu'

Nehemiah 1:3

Wakaniambia

Hapa "Wao" hutaanisha Hanani na watu wengine ambao walikuja kutoka Yuda.

jimbo

Hapa "jimbo" linamaanisha Yuda kama wilaya ya utawala chini ya Dola ya Kiajemi. AT "jimbo la Yuda" au "Yuda"

ukuta wa Yerusalemu umebomolewa na milango yake imeteketezwa kwa moto

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. Majeshi ya "AT wamevunja ukuta wa Yerusalemu na kuweka milango yake kwa moto"

Nehemiah 1:4

kisaha akasema

Nehemiya anasema yale aliyoomba. AT "Ndipo nikamwambia Bwana"

wale wanaokupenda na kushika amri zake

Kwa kuwa Nehemia anazungumza na Yahweh, matamshi "yeye" na "yake" yanaweza kutafsiriwa kama "wewe" na 'yako." AT "ambaye anakupenda na kushika amri zako"

Nehemiah 1:6

fungua macho yako

Nehemiya anasema kama Mungu anamtazama yeye akipenda kama Mungu angepoufungua macho na kumtazama. AT "kuangalia mimi' au 'makini na mimi"

ili uweze kusikia sala ya mtumishi wako

"ili uisikie maombi ambayo mimi, mtumishi wako, ninaomba." Neno 'mtumishi' linamaanisha Nehemia. Hii ndivyo mtu anavyoweza kumtambulisha mkuu wake ili kuonyesha unyenyekevu na heshima.

mchana na usiku

Kwa kusema kwamba anaomba wote wakati wa mchana na wakati wa usiku, Nehemia anasisitiza mzunguko wa sala zake. AT "wakati wote"

Wote mimi na nyumba ya baba yangu

Hapa neno "nyumba" linawakilisha familia. AT "Wote mimi na familia yangu"

Nehemiah 1:8

Taarifa ya unganisha

Nehemia anaendelea kuomba kwa Mungu.

Tafadhali kumbuka nia

"Kumbuka nia" ni dhana ambayo ina maana kukumbuka. AT 'Tafadhali kumbuka'

neno ulilomuamuru mtumishi wako Musa

Matamshi "wewe" na "yako" kinamaanisha Mungu.

mkitenda pasipo uaminifu... nitawatawanya ....lakini mkirudi ...watu wako

Matamshi "'wewe" na "yako" ni wingi na hutaja watu wa Israeli.

itawatawanya kati ya mataifa

Bwana anaongea ya kuwafanya Waisraeli wapate kuishi katika mataifa mengine kama kwamba aliwatangaza wao kama mtu atakayegawa mbegu. AT '"itawafanya uishi kati ya mataifa'"

ingawa watu wako walienea

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT 'ingawa nimewatangaza watu wako'

chini ya mbingu za mbali

Bwana anasema juu ya maeneo duniani ambayo ni mbali sana kama "chini ya mbingu za mbali." AT "kwenda mahali mbali sana"

mahali pale nilichochagua ... kubaki

Maneno haya yanamaanisha Yerusalemu, ambako hekalu lilikuwa iko. AT "kwenda Yerusalemu, ambapo nimechagua ... kubaki'"

ambapo nimechagua kufanya jina langu kubaki

Hapa neno "jina" linawakilisha Bwana mwenyewe. AT "ambapo nimechagua kukaa"

Nehemiah 1:10

Taarifa za jumla

Nehemia anaendeleza maombi yake

Sasa

Neno hili linatumika hapa kuashiria mapumziko katika sala ya Nehemia. Hapa anaanza kufanya ombi lake kulingana na ahadi ya Bwana.

wao ni watumishi wako

Neno "wao" linamaanisha watu wa Israeli.

kwa nguvu yako kubwa na kwa mkono wako wenye nguvu.

Hapa "mkono" inawakilisha nguvu au nguvu. Pamoja, maneno haya mawili huunda doublet ambayo inasisitiza ukubwa wa nguvu za Bwana. AT "kwa uwezo wako mkubwa na kwa nguvu yako ya nguvu" au "kwa uwezo wako wenye nguvu sana"

sala ya mtumishi wako

Hapa "mtumishi" inahusu Nehemia. Hii ndivyo mtu anavyoweza kumtambulisha mkuu wake ili kuonyesha unyenyekevu na heshima. Tazama jinsi ulivyotafasiri hii katika 1: 6.

sala za watumishi wako

Hapa "watumishi" inawakilisha watu wengine wa Israeli ambao wangekuwa wakiomba kwa Yahweh kutenda kwa niaba ya watu wake na kwa niaba ya Yerusalemu.

ambao hufurahia kuheshimu jina lako

Hapa "jina" linawakilisha Yahweh mwenyewe. AT 'ambaye anapenda kukuheshimu'

unijalie rehema mbele ya mtu huyu

Hapa "yeye" inaongelea Nehemia, ambaye anajielezea mwenyewe katika mtu wa tatu kuonyesha ubinafsi wake mbele ya Mungu, na "mtu huyu" ana maana ya Artaxerxes, mfalme wa Persia.

mbele ya mtu huyu

Nehemiya anasema mtazamo au mtazamo wa mfalme kama ilivyokuwa jinsi mfalme alivyoona kitu fulani. AT"'ruzuku kwamba mfalme atanihurumia"

Nilikuwa mnyweshaji wa mfalme

Nehemiya anasema mtazamo au mtazamo wa Hii ni habari ya historia kuhusu nafasi ya Nehemiya katika mahakama ya mfalme. Lugha yako inaweza kuwa na njia maalum ya kuandika taarifa ya nyuma.

Nehemiah 2

Nehemiah 2:1

Katika mwezi wa Nisani

"Nisani" ni jina la mwezi wa kwanza wa kalenda ya Kiebrania.

katika mwaka wa ishirini wa mfalme Artashasta

"mwaka wa 20 ambao Artashasta alikuwa mfalme"

Sasa

Neno hili linatumika hapa kuashiria mapumziko katika hadithi kuu. Hapa Nehemiya anasema maelezo ya habari juu ya tabia yake mbele ya mfalme.

Lakini mfalme

"hivyo mfalme"

Kwa nini uso wako una huzuni

Hapa Nehemia anajulikana kwa uso wake kwa sababu uso unaonyesha hisia za mtu. AT "Kwa nini wewe huzuni sana"

Hii lazima iwe huzuni ya moyo

Hii inazungumzia Nehemia kuwa huzuni kama moyo wake ulikuwa na huzuni, kwa kuwa moyo mara nyingi huonekana kuwa katikati ya hisia. AT "Lazima uwe mwenye huzuni sana"

Nehemiah 2:3

Mfalme aishi milele!

Nehemia anaonyesha heshima kwa Mfalme Artashasta. Hapa "milele" ni kisingizio kinachoashiria maisha ya muda mrefu. "Mfalme aishi muda mrefu!" au "Mfalme awe na maisha marefu!"

Kwa nini uso wangu usiwe na huzuni?

Hapa Nehemiya anatumia swali hili la uongo ili kumwambia mfalme kwamba ana sababu ya kuwa na huzuni. Hii inaweza kuandikwa kama taarifa. AT 'Nina sababu nzuri sana za kuwa na huzuni.'

mji wa kaburi za baba zangu

"mahali ambapo baba zangu wamezikwa"

malango yake yameharibiwa kwa moto

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "moto umeangamiza milango yake" au "adui yetu amewaka moto milango yake"

Nehemiah 2:4

Nikamwambia mfalme

"Kisha nikamjibu mfalme"

mtumishi wako

Nehemia anajieleza mwenyewe njia hii ya kuonyesha utii wake kwa mfalme.

Mbele yako

Hapa mbele inawakilisha hukumu au tathmini. AT 'katika hukumu yako'

mji wa kaburi za baba zangu

"mji ambapo baba zangu wamezikwa"

ili nipate kuujenga

Nehemia haina mpango wa kujenga jengo lote mwenyewe, lakini atakuwa kiongozi wa kazi hiyo. AT "kwamba mimi na watu wangu wanaweza kujenga tena"

Nehemiah 2:7

Naweza kupewa barua

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "unaweza kutoa barua kwangu"

Jimbo ng'ambo ya mto

Hii ndiyo jina la jimbo ambalo lilikuwa magharibi ya Mto Efrati. Ilikuwa ng'ambo ya mto kutoka mji wa Susa.

Asafu

Hili ndio jina la mtu.

mkono mzuri wa Mungu ulikuwa juu yangu

"Mkono mzuri" wa Mungu unawakilisha "neema yake." AT "neema ya Mungu ilikuwa juu yangu"

Nehemiah 2:9

Sanbalati Mhoroni ......... Tobbia

Sanbalati ni jina la mtu, na Wahoroni walikuwa kikundi cha watu.

Tobbia mtumishi wa Amoni

Huyu mtu huenda alikuwa mtumwa aliye huru sasa akiwa kama afisa katika Amoni.

kusikia hii

"kusikia kwamba nimekuja" (UDB)

Nehemiah 2:11

alichoweka ndani ya moyo wangu

Hapa "moyo" Nehemia inahusisha mawazo na mapenzi yake. AT "alikuwa ameongoza kwangu' au 'aliniongoza"

Hakukuwa na mnyama pamoja nami

'Hakuna kulikuwa na wanyama pamoja nami'

Nehemiah 2:13

Taarifa za jumla

Wanaume wachache waliongozana Nehemia kwenye ukaguzi huu, lakini anaongea kwa mtu wa kwanza kwa sababu alikuwa mtu wa kwanza.

Niliondoka usiku kwa njia ya lango la bondeni

"Usiku, nilitoka kupitia Bonde la Bonde"

Joka

mbwa mwitu

mrango wa siri

Inawezekana, kukataliwa kuliondolewa kutoka kwa jiji kupitia lango hili.

ambazo zimebomolewa, na milango ya mbao iliharibiwa na moto

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "ambayo maadui wa Israeli walikuwa wamevunjika wazi, na milango ya mbao ambayo maadui wao waliharibu kwa moto"

Nehemiah 2:15

Hivyo nilikwenda ...... na nikarudi

Wanaume wengine pamoja na Nehemia walimfuata pia. AT 'Hivyo tulikwenda ... na tukageuka

wa lango la bondeni

"kwa njia ya lango la bonde"

wengine waliofanya kazi hiyo

Hii inahusu wanaume ambao baadaye watajenga kuta. AT "wengine ambao baadaye watafanya kazi ya kujenga upya"

Nehemiah 2:17

Munaona shida

Hapa "ni" wingi, akimaanisha watu wote waliotajwa katika 2: 15.

milango yake imeharibiwa kwa moto

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "jinsi adui zetu walivyoharibu milango yake kwa moto"

hivyo hatuwezi tena kuwa na aibu

"hivyo hatuwezi tena kuona aibu"

mkono mzuri wa Mungu wangu ulikuwa juu yangu

'Mkono mzuri" wa Mungu unawakilisha "neema yake." AT "neema yangu Mungu ilikuwa juu yangu"

kuinuka na kujenga

Huu ndio idiami. AT "kuanza kujenga'"

Kwa hiyo wakaimarisha mikono yao kwa ajili ya kazi nzuri.

Maneno ya "kuimarisha mikono yao" inamaanisha kujiandaa kufanya kitu. AT "Hivyo wameandaa kufanya kazi hii nzuri"

Nehemiah 2:19

Sanbalati.... Tobia

Haya ni majina ya watu. Tafsiri kama 2:9

Geshemu

Hili ni jina la mtu.

Unafanya nini? Je! Unagombana na mfalme?

Maswali haya ya kihistoria hutumiwa kumshtaki Nehemia. Hizi zinaweza kuandikwa kama taarifa. AT "Wewe unafanya upumbavu! Usipaswi kupigana na mfalme! "

Mfalme

Hii inahusu Artaxerses, mfalme wa Persia.

tutaondoka na kujenga

Huu ndio idiami. AT 'itaanza upya'

Lakini huna sehemu, hakuna haki, na hakuna dai la kihistoria huko Yerusalemu

'"akini huna sehemu, haki ya kisheria, au dai la kidini kwa Yerusalemu"

Nehemiah 3

Nehemiah 3:1

Kisha Eliashibu, kuhani mkuu, akasimama pamoja na ndugu zake makuhani

Kisha Eliashibu, kuhani mkuu, akaja pamoja na ndugu zake, makuhani

Eliashibu....Zakuri mwana wa Imri

Haya nim majina ya watu.

Mnara wa Mia

"Mnara wa 100"

Mnara wa Hamea

Hili ndio jina la mnara. Inawezekana kuitwa jina la mtu aliyeitwa '"Hamea"

watu wa Yeriko

Hii ina maana kwamba watu walikuwa kutoka Jeriko. AT "watu kutoka Jeriko"

Nehemiah 3:3

Hasena....Meremothi... Uria...Hakosi...Meshulamu ...Berekia...Meshezabeli...Sadoki... Baana

Haya ni majina ya watu

kuweka milango yake

"ameweka milango yake" au "kuweka milango yake mahali"

vyuma vyake na makomeo yake

"kufuli na baa zake." Hizi zimefungwa malango salama.

Meremoth aliandaa sehemu inayofuata.....Meshulamu akatengeneza....Sadoki akatengeneza. ...Watekoi wakatengeneza

Maneno haya yanataja kutengeneza ukuta. AT "Meremoti alipanda sehemu inayofuata ya ukuta ... Meshullam alipanda ukuta ... Sadoki alipanda ukuta ... Tekoites alipanda ukuta"

Watekoi

Hawa ni watu kutoka mji wa Tekoa.

iliyoagizwa na wakuu wao

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "kwamba wasimamizi wao waliwaamuru wafanye"

Nehemiah 3:6

Yoyada...Pasea na Meshulamu...Besodeya...Melatia...Yadoni

Haya ni majina ya watu

kuweka milango yake

"ameweka milango yake" au "kuweka milango yake mahali"

vyuma vyake na makomeo yake

"kufuli na komeo zake." Hizi zimefungwa malango kwa usalama.

Gibeoni...Meronothi

Wagibeoni na Meronothi ni makundi ya watu.

Gibeoni na Mispa

Haya ni majina ya mahali

mkoa wa ng'ambo ya Mto

Hili ndiyo jina la mkoa ambao lilikuwa magharibi ya Mto Efrati. Ilikuwa ng'ambo ya mto kutoka mji wa Susa. Tafsiri kama katika 2:7.

Nehemiah 3:8

Uzieli...Harhaya...Hanania...Refaya....Huri... Yedaya...Harumafu...Hatushi ...Hashabneya

Haya ni majina ya watu

mfuadhahabu

Mfuadhahabu ni mtu anayefanya mapambo ya dhahabu na vitu vingine vya dhahabu.

wafuadhahabu, Huru alijenga ukuta ... Harumafu alijenga ukuta ... Hashabneiah alijenga ukuta

Maneno haya yanataja kujenga ukuta. wafuadhahabu, walijenga ukuta ... Huru alijenga ukuta ... Harumaph alijenga ukuta ... Hashabneiah alijenga ukuta "

baada yake Hanania, mtengenezaji wa manukato

Hanania alijenga ukuta pia. AT "baada yake Hananiah, mtengeneza manukato, alijenga ukuta"

manukato

kimiminika kioevu ambazo watu huvaa mwili wao kwa kiasi kidogo cha harufu nzuri

mtawala

"msimamizi mkuu"au "kiongozi"

nusu ya wilaya

"Nusu" ina maana sehemu moja kati ya sehemu mbili sawa.

Nehemiah 3:11

Malkiya...Harimu....Hashubu...Pahat Moabu...Shalumu.....Haloheshi

Haya yote ni majina ya watu

wajenga sehemu nyingine...alijenga, pamoja na binti zake.

Maneno haya yanataja ukarabati wa ukuta. AT "walijenga sehemu nyingine ya ukuta ... alijenga ukuta, pamoja na binti zake"

Shalumu mwana wa Haloheshi, mtawala

Sharumu alikuwa mtawala, sio Halloheshi.

mtawala

"msimamizi mkuu" au "kiongozi"

nusu ya wilaya

"Nusu" ina maana sehemu moja kati ya sehemu mbili sawa.

Nehemiah 3:13

Hanuni

Hili ni jina la mtu

wenyeji wa Zanoa

"watu kutoka Zanoa"

Zanoa

Hili ndiyo jina la mahali

Lango la Bonde

"Lango la Bonde" au "Lango Lenye Upeleka Bonde" Jaribu kutafsiri maneno haya kama jina, si kama maelezo.

kuweka milango yake

"imeweka milango yake" au "kuweka milango yake mahali"

vyuma vyake na makomeo yake

"kufuli na makomeo yake." Hizi zimefungwa malango salama.

Walijenga dhiraa elfu hadi lango la jaa.

Walijenga sehemu ya ukuta kati ya lango la Bonde na lango la jaa. AT "Walitengeneza dhiraa elfu za ukuta, kutoka kwenye mlango wa bonde hadi kwenye lango la jaa"

Walitengeneza dhiraa elfu

Maneno ya kukosekana "ya ukuta" yanaweza kuongezwa. AT "Walitengeneza dhiraa elfu za ukuta" "Wakajenga dhiraa elfu nyingine za ukuta ulio ng'ambo ya lango la Mtaa"

dhiraa elfu

"Dhiraa 1,000." Hii inaweza kuandikwa kwa vipimo vya kisasa. AT "mita 460"

Lango la jaa

Inawezekana, kukataliwa kuliondolewa kutoka kwa mji kupitia lango hili. Jaribu kutafsiri maneno haya kama jina, sio tu kama maelezo.

Nehemiah 3:14

Malkiya.... Rekabu.....Shalumu...Kolhoze

Haya ni majina ya watu

Malkiya, mwana wa Rekabu, mtawala

Malkiya alikuwa mtawala, alikuwa hapatikani.

mtawala

"msimamizi mkuu" au "kiongozi"

Beth-Hakeremu

Hili ni jina la sehemu

yeye ......kuweka milango yake

"aliweka milango yake" au "akaweka milango yake mahali"

vyuma vyake na makomeo yake

"kufuli na baa zake." Hizi zimefungwa malango salama.

Shalumu mwana wa Kolhoze, mtawala

Shalumu alikuwa mtawala, sio Kolhoze

ukuta wa Pwani wa Silowamu

Hii inamaanisha kuwa ukuta ulikuwa karibu na Pwani la Siloamu. AT "ukuta uliozunguka Pwani la Siloamu"

Nehemiah 3:16

Nehemia mwana wa Azbuki, mtawala

Nehemia alikuwa mtawala, si Azbuki.

Nehemia

Huyu ni mtu tofauti aitwaye Nehemia kutoka kwa mtu aliyeandika kitabu hiki.

mtawala

"msimamizi mkuu" au "kiongozi"

nusu ya wilaya

"Nusu" ina maana sehemu moja kati ya sehemu mbili sawa

Nehemia...Azbuki...Rehumi....Hashabia

Haya ni majina ya watu.

Beth-suri...Keila

Haya ni majina ya mahali

kujenga mahali... Walawi walijenga

Maneno haya yanataja kutengeneza ukuta. AT "aliandaa ukuta hadi mahali ... Walawi walijenga ukuta"

watu wenye nguvu

"wapiganaji"

kwa wilaya yake

"anayewakilisha wilaya yake" au "kwa niaba ya wilaya yake"

Nehemiah 3:18

Baada yake

"Karinu yake"

watu wa nchi zao walijenga..... wakajenga sehemu nyingine

Maneno haya yanataja kutengeneza ukuta. AT 'Kisha yake watu wa nchi walijenga ukuta ... waliandaliwa sehemu nyingine ya ukuta'

Bavai...Henadadi...Ezeri...Yeshua

haya ni majinam ya watu.

Bivai mwana wa Henadadi, mtawala

Bavvai alikuwa mtawala, si Henadad.

Keila.......Mispa

Haya mi majina ya mahali.

Ezeri mwana wa Yeshua, mtawala

Ezeri alikuwa mtawala, sio Yeshua

kuelekea upande wa silaha

"mbele ya hatua zilizotokea kwenye silaha'"(UDB)

ghala

mahali ambapo silaha zinahifadhiwa

Nehemiah 3:20

Baada yake

"Karibu na yeye"

aruki....Zakai...Eliashibu......Meremothi....Uria....Hakosi

Haya ni majina ya watu

akajenga sehemu nyingine

Hii inahusu kutengeneza ukuta. AT "iliandaa sehemu nyingine ya ukuta"

Nehemiah 3:22

karibu na Yerusalemu, walijenga.....Benyamini na Hashubu walijenga.....Azaria alijenga.... alijenga

Maneno haya yanataja kutengeneza ukuta. "Kote Yerusalemu, kujenga ukuta ... Hashubu alijenga ukuta ... Azaria alijenga ukuta ... Binnui alijenga ukuta"

Benyamini...Hashubu......Azaria....Maaseya....Anania.... Binui.....Henadadi

haya ni majina ya watu.

kuielekea nyumba yao

"mbele ya nyumba yao"

Baada yao.... Baada yake

"Karibu nao...... Karibu nae"

Nehemiah 3:25

Palali...Uzai.....Pedaya.....Paroshi

Haya ni majina ya watu

Uzai akajenga....Paroshi akajenga... watumwa wakajenga...wakajenga sehemu nyingine

Maneno haya yanataja kutengeneza ukuta. AT "Uzai alijengaa ukuta ... Paroshi alijenga ukuta ... watumishi walijenga ukuta ... walijenga sehemu nyingine ya ukuta"

Baada yake

"Karibu naye"

mnara unaoenea juu

"mnara unaoinuka"

nyumba ya juu ya mfalme

"nyumba ya juu ya kiongozi wa Israeli"

uwanda wa walinzi

Hii ndio mahali ambapo walinzi walikaa

Ofeli

Hiii ni jina la mahali.

karibu na lango la maji

mbele ya lango la maji

mnara unaojitokeza ... mnara mkubwa unaojitokeza

"mnara mrefu ... mnara mrefu." Maneno "mnara unaojitokeza" inamaanisha mnara mrefu ambao unaruka kutoka kwenye ukuta. Inawezekana kwamba maneno haya yote yanataja mnara huo.

Watekoi

Hawa ni watu kutoka mji wa Tekoa. Tafsiri hii sawa na ulivyofanya katika 3:3.

Nehemiah 3:28

makuhani wakajenga.... wakajenga sehemu..... mlango wa mashariki... tengeneza.... wakajenga sehemu nyingine ya ukuta.... wakajenga kuelekea

Maneno haya yanataja kutengeneza ukuta. "makuhani walitengeneza ukuta ... walitengeneza sehemu ya ukuta ... mlango wa mashariki, ukarabati wa ukuta ... ukarabati sehemu nyingine ya ukuta ... ukarabati ukuta kinyume"

Juu ya lango la farasi

Neno "juu" linatumika hapa kwa sababu nyumba za makuhani zilikuwa ziko kwenye mwinuko wa juu zaidi kuliko lango la farasi.

kuelekea nyumba yake

"mbele ya nyumba yake"

Baada yao ... Baada yake

"Karibu nao ... karibu naye"

Sadoki... Imeri....Shelemia...Shekania....Hanania..Shekania....Hanuni..Salafu.... Meshulamu.....Berekia

Haya ni majina ya watu

Shemaya mwana wa Shekania, mlinzi wa lango la mashariki

Shemaya alikuwa mlinzi wa mlango wa mashariki, si Shekania

mlinzi wa lango la mashariki

"mtu aliyeangalia lango wa mashariki" au "mtu ambaye alifungua na kufunga mlango wa mashariki"

mwana wa sita

"mwana wa 6"

kuelekea kwenye vyumba vyake

"mbele ya vyumba ambako alikaa." Neno "wake" linamaanisha Meshullam.

Nehemiah 3:31

Baada yake

"Aliyefuata baada yake"

Malkiya

Hlii ni jina la mtu.

wafua dhahabu

Mfua dhahabu ni mtu anayefanya mapambo ya dhahabu na vitu vingine vya dhahabu.

iliandaliwa kwa nyumba ... wafanyabiashara walijenga

Maneno haya yanataja kutengeneza ukuta. AT "waliandaa ukuta kwa nyumba ... wafanyabiashara walijenga ukuta"

wafanyabiashara

"wauzaji" au "wafanyabiashara"

chumba cha juu cha pembeni

vyumba vya ngazi ya juu ambapo watu walikaa

Lango la Kondoo

Hili ni jina la mlango wa ukuta.

Nehemiah 4

Nehemiah 4:1

Sasa pindi Sanbalati

Hapa Nehemia anatumia neno 'sasa' kuashiria sehemu mpya ya hadithi.

Sanbalati.... Tobia

Hiya ni majina ya wanaume. Tafsiri kama 2:9

akaghadhabika ndani yake, naye akakasirika sana

Hapa "ina maana ya kutambua kwa Sanballat kwamba Wayahudi wanajenga kuta. Hii inazungumzia Sanballat kuwa mwenye hasira sana kama hasira yake ilikuwa moto mkali. AT "alikasirika sana' au 'alikasirika sana"

Mbele ya ndugu zake

"Mbele ya ndugu zake" au "mbele ya ndugu yake"

Kwa nini ni wadhaifu..... wataweza kurejesha...watatoa dhabihu...wataimaliza kazi kwa siku?

Sanibalati anauliza maswali haya kuwacheka Wayahudi. Hizi zinaweza kuandikwa kama taarifa. AT "Wayahudi dhaifu hawawezi kufikia chochote. Hawawezi kurejesha mji kwao wenyewe. Hawatatoa dhabihu. Hawatamaliza kazi siku."

Wayahudi dhaifu

"Wayahudi dhaifu"

kwa siku

Hii inazungumzia ya kumaliza kitu haraka kwa kusema kwamba haiwezi kukamilika siku. AT "haraka"

Watawaletea mawe kutoka kwenye kifusi baada ya kuchomwa moto?

Sanbalati pia huuliza swali hili kuwacheka Wayahudi. Hii inaweza kuandikwa kama taarifa. AT 'Hawatawafufua tena mawe kutoka kwa makundi ya shida yaliyotumika.'

Watawaletea mawe kutoka kwenye kifusi baada ya kuchomwa moto

Hii inazungumzia watu kujenga upya jiji kama kwamba walikuwa wakimrudisha. AT "kurejesha mji na kujenga upya kuta zake kwa mawe yasiyofaa ambayo yalikuwa yamekotengenezwa na akageuka kuwa shida"

kutoka kwenye kifusi baada ya kuchomwa moto

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "kutoka kwa matundu ya shida ambayo mtu alikuwa amekwisha"

Ikiwa tu mbweha angepanda juu ya hichi wanachokijenga, angeubomoa ukuta huo wa mawe

Sanbalati hudhihaki ukuta na kueneza jinsi ilivyo dhaifu kwa kusema kwamba mbweha inaweza kuiangusha. AT "Ukuta huo wanaojenga ni dhaifu sana hata hata kama mbweha mdogo ulipanda juu yake, ukuta wao wa jiwe ungeanguka chini" (UDB)

Nehemiah 4:4

Tusikilize, Mungu wetu,....kwa sababu wamewashawishi wajenzi kuwa na hasira

Hapa Nehemiya anaomba kwa Mungu. Hii inaweza kuelezwa wazi na imeandikwa kwa alama za nukuu. AT 'Kisha nikasali,' Sikilizeni, Mungu wetu, ... kwa sababu wamewashawishi wajenzi kuwa na hasira ''

Tusikilize, Mungu wetu, kwa maana sisi tunatukanwa

Hapa neno "sisi" linamaanisha Wayahudi. Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "Sikilizeni, Mungu wetu, kwa kuwa maadui wetu wanatudharau."

kuwapa wapate kutekwa

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT 'waache adui zao kuwaibia'

disha malalamiko yao juu ya vichwa vyao wenyewe

Maneno "malalamiko yao" yanamaanisha matusi ya Sanibalati na Tobia. Hapa neno 'vichwa' linamaanisha watu wote. AT "Turn their taunts juu yao wenyewe" au "Sababu maneno yao ya kudharau kujichea wenyewe"

Usiufunike

Hii inazungumzia dhambi za kusamehe za mtu kama kitu ambacho kinaweza kujificha kimwili. AT "Usisamehe"

wala usiondoe dhambi zao mbele yako

Hii inazungumzia kusahau dhambi za mtu kama kwamba ni kitu kilichoandikwa ambacho kinaweza kufutwa. AT "usisahau dhambi zao"

kwa sababu wamewachukiza wanaojenga

"wamekasirika wajenzi"

Kwa hiyo tulijenga ukuta

"Hivyo tukajenga upya"

ukuta wote uliunganishwa kwa nusu ya urefu wake

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "tuliunganisha ukuta pamoja na ilikuwa nusu urefu wake wote"

nusu ya ulefu wake

"Nusu" ina maana sehemu moja kati ya sehemu mbili sawa.

Nehemiah 4:7

ghadhabu kubwa ikawaka ndani yao

Hii inazungumzia watu kuwa wenye hasira sana kama hasira yao ilikuwa kitu ambacho kilichomwa ndani yao. AT "walikasirika sana" au "walikasirika"

dhidi ya Yerusalemu

Hapa "Yerusalemu" inahusu watu wanaoishi huko. AT "dhidi ya watu wa Yerusalemu"

kuweka walinzi kama ulinzi

"kuweka watu karibu na ukuta kulinda mji" (UDB)

Nehemiah 4:10

Kuna kifusi kikubwa

KIfusi ni "jiwe la kuteketezwa" au 'jiwe lililovunjika' au 'jiwe lisilowezekana.'

Wala hawatajua au kuona mpaka tutakapokuja kati yao

'"Hawatatuona tukija mpaka tutakapokua karibu nao"

Nehemiah 4:12

kutoka pande zote

Hii inawakilisha pande zote. Neno "zote" linawakilisha "wengi." AT "kutoka maelekezo mengi"

kuzungumza nasi mara kumi

Hapa namba 10 hutumiwa kuwakilisha "wengi.' AT "kuzungumza nasi mara nyingi"

katika sehemu zilizo wazi

"katika maeneo magumu"

Niliweka kila familia

Hii inahusu watu kadhaa kutoka kwa kila familia, hii inawezekana haijumuishi wanawake na watoto. AT "niliweka watu kutoka kila familia"

mkumbukeni Bwana

maneno "wito kwa akili" inamaanisha kukumbuka. AT "Mkumbuka Bwana"

Nehemiah 4:15

Ilipokuwa wakati

"ikatokeae kwamba"

mipango yao ilikuwa inayojulikana kwetu

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "tulijua kuhusu mipango yao"

watumishi wangu walifanya kazi

"watumishi wangu walifanya kazi"

nusu ya watumishi wangu .... nusu kati yao

"Nusu" ina maana sehemu moja kati ya sehemu mbili sawa.

viongozi walisimama nyuma ya watu wote

"viongozi walijiweka wenyewe nyuma ya watu wote"

Nehemiah 4:17

Kila mtu alifanya kazi kwa mkono mmoja, na kwa mkono mwingine alikuwa na silaha yake

Hii ni kisichozidi. Hawakuwa na kazi kwa mkono mmoja tu, lakini daima walikuwa na silaha yao pamoja nao ili wawe tayari kujikinga na wale walio karibu nao.

Nehemiah 4:19

Nikasema

Hapa "mimi" inahusu Nehemia.

wakuu.... wakuu

Hawa ndio viongozi waliotajwa katika 4:15.

Kazi ni kubwa

Hapa neno "kubwa" lina maana "kubwa" au "kubwa."

sauti ya tarumbeta

Hii inahusu mtu anayepiga tarumbeta. AT "mtu anapiga tarumbeta"

Nehemiah 4:21

nusu yao

"Nusu" ina maana sehemu moja kati ya sehemu mbili sawa.

kutoka kupambazuka asubuhi hadi kutokea kwa nyota

Hii inahusu siku nzima, wakati ni mwanga nje. AT "kutoka mwanga wa kwanza wa siku mpaka mwanzo wa usiku"

kupambazuka asubuhi

Ni hatua kwa wakati ambapo jua huchomoza ambayo ni "asubuhi." AT "kupanda kwa jua" au "asubuhi"

katikati ya Yerusalemu

"ndani ya Yerusalemu"

kubadirisha nguo zetu

akaondoa nguo zetu

Nehemiah 5

Nehemiah 5:1

Kisha wale wanaume na wake zao wakalia kwa nguvu dhidi ya Wayahudi wenzao

Kwa kuwa walikuwa wakifanya kazi juu ya ukuta, wafanyakazi hawakuwa na muda wa kutosha wa kufanya kazi kununua na kukua chakula kwa familia zao. Maana kamili ya kauli hii yanaweza kufanywa wazi.

wanaume na wake zao

Hii inahusu wanaume waliokuwa wakijitahidi kujenga jengo.

wakapaza kilio kikubwa

"Sauti" inaweza kuelezewa kama kitenzi. AT "alilia kwa sauti kubwa"

Tunaweka rehani mashamba yetu

"Tunapaswa kutoa ahadi" au "Tunapaswa kutoa katika ahadi"

Nehemiah 5:4

Hata hivyo sasa miili yetu na damu ni sawa na ndugu zetu, na watoto wetu ni sawa na watoto wao

Hapa Wayahudi wanasema kuwa wao ni wa Kiyahudi sawa na Wayahudi wengine na kwamba wao ni wa umuhimu sawa na wengine. Maana ya hili yanaweza kufanywa wazi. AT "Hata hivyo familia zetu ni Wayahudi kama familia za Wayahudi wengine, na watoto wetu ni muhimu tu kwetu kama watoto wao ni wao"

miili yetu na damu

Hii ni idiamu ambayo inahusu wanafamilia wao. AT "familia yetu"

Baadhi ya binti zetu tayari wamekuwa watumwa

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "Tumewauza baadhi ya binti zetu katika utumwa"

Lakini hatuna nguvu za kusaidia kwa sababu watu wengine sasa wana mashamba yetu na mizabibu yetu."

Kwa vile shamba la mens na mizabibu hazimiliki, hawawezi kuzalisha pesa wanazohitaji kusaidia familia zao. Nia kamili ya hii inaweza kufanywa wazi. AT "Lakini hatuwezi kubadilisha hali hii kwa sababu wanaume wengine sasa wana mashamba yetu na mizabibu tunayohitaji ili kuunga mkono maisha yetu."

sio katika uwezo wetu

Hii ni idiom ambayo ina maana kwamba hawana rasilimali za kufanya kitu. AT "hatuwezi"

Nehemiah 5:6

niliposikia kilio chao

"Sauti" inaweza kuelezewa kama kitenzi. AT "wakati niliposikia wanapiga kelele"

Ninyi mnatafuta riba, kila mmoja kutoka kwa ndugu yake mwenyewe

Kila Myahudi angejua kwamba ni makosa chini ya Sheria ya kulipa riba kwa Myahudi mwingine. Nia kamili ya hii inaweza kufanywa wazi. AT 'Kila mmoja wenu anatoa riba kwa ndugu yako mwenyewe, na hiyo ni sahihi chini ya Sheria'

Nikakutanisha kusanyiko kubwa juu yao

Hii ina maana kwamba alikusanya kundi kubwa la watu na kuletwa mashtaka haya dhidi yao. Maana ya maneno haya yanaweza kufanywa wazi. AT 'nilikuwa na kusanyiko kubwa na kuwaleta mashtaka haya dhidi yao' au 'niliwashikilia kesi mbele ya mkutano'

akini hata mnawauza ndugu na dada zenu ili wauzwe tena kwetu

Hii ina maana kwamba wanauza wanachama wa familia zao kuwa watumwa kwa Wayahudi wenzake. Maana kamili ya kauli hii yanaweza kufanywa wazi. AT "Sasa unauza watu wako kuwa watumwa wa Wayahudi wenzako, ili baadaye waweze kuuzwa kwetu tena"

nani ambao walikuwa wameuzwa kwa mataifa

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "ambao watu waliuzwa kama watumwa kwa mataifa"

Nehemiah 5:9

Pia wakasema

Herufi "I" inamhusu Nehemia

Mnachokifanya

"Wewe" hapa inawakilisha wakuu wa Kiyahudi.

Je, hampaswi kutembea katika hofu ya Mungu wetu ili kuzuia malalamiko ya mataifa ambayo ni adui zetu?

Huu ndio swali la uhubiri ambalo Nehemia anatumia kuwapiga wakuu. Inaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Unapaswa kutembea katika hofu ya Mungu wetu ili kuzuia malalamiko ya mataifa ambayo ni adui zetu."

kutembea katika hofu ya Mungu wetu

Hii ni ya kupendeza. Hapa "kutembea" inahusu tabia ya mtu na njia anayoishi. AT "uishi maisha yako kwa njia ambayo humtukuza Mungu."

malalamiko ya mataifa ambayo ni adui zetu

Neno "kutulalamikia" linamaanisha "udanganyifu" au "dhihaka" na inaweza kuelezwa kama kitenzi. AT "mataifa ambao ni maadui wetu kwa kutulalamikia" au "mataifa ya adui kudhihaki"

kuwapa

kukopa au kutoa kitu kwa mtu anayetarajia ulipaji

mkopo

Hii ni pesa, chakula, au mali ambayo mtu mmoja anaweza kuruhusu mtu mwingine akope ili kulipa madeni. Wakopaji basi atakuwa na deni kwa mkopeshaji.

asilimia

Sehemu ya thamani ya mkopo ambayo akopaye atadaiwa kwa riba.

wewe ulitaka kutoka kwao

'uliwadai" au "uliwafanya kulipa"

Nehemiah 5:12

Kisha wakasema

Hapa "wao" inawakilisha viongozi wa Kiyahudi.

Tutarudisha kile tulichochukua kutoka kwao

Viongozi wa Kiyahudi wanasema watarudi fedha ambazo Wayahudi masikini walilipwa kwa mashtaka

kuwaapisha kuwafanya

Hapa neno "wao" linamaanisha viongozi wa Kiyahudi.

Ndipo nikawaita

"Mimi" inahusu Nehemiya.

Nikakung'uta vazi langu

'Nilitupa mifuko ya vazi langu.' Mara nyingi katika Agano la Kale, viapo vilivyoonyeshwa kama ushahidi kwa yale aliyoahidiwa. Nehemia anawaonyesha viongozi wa Kiyahudi nini kitatokea ikiwa watavunja ahadi waliyoifanya.

Kwa hiyo Mungu awaondoe katika nyumba yake....... Kwa hiyo akung'utwe na kuwa hana kitu

Hapa Nehemia anasema juu ya Mungu akiondoa mali yote ya mwanadamu kama kwamba Mungu alikuwa akimfukuza nje ya nyumba yake na mali kama Nehemia alivyokuwa amekung'uta vazi lake. AT "Kwa hiyo Mungu aondoe kwa kila mtu asiyeweka ahadi yake yote mali yake na nyumba yake kama nimechukua kila kitu nje ya kifuniko cha nguo yangu"

Nehemiah 5:14

tangu wakati niliowekwa

Hapa "mimi" inahusu Nehemia.

tangu mwaka wa ishirini mpaka mwaka wa thelathini na pili

mwaka wa pili - "tangu mwaka wa 20 hadi mwaka wa 32"

wa mfalme Artashasta

Artashasta alikuwa mfalme

chakula kilichotolewa kwa gavana

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "walikula chakula ambacho watu walitoa kwa gavana"

kwa kila siku

"kila siku kwa ajili yao"

wakuu wa zamani

wakuu wa zamani au "magavana wa zamani." Nehemia hakuwa gavana wa kwanza wa Yuda.

Shekeli Arobaini

"Shekeli 40" au "sarafu za fedha 40" (UDB).

Lakini sikufanya hivyo kwa sababu ya hofu ya Mungu.

"Lakini kwa sababu hofu yangu ya Mungu sikuchukua chakula" au "Lakini sikuwa na chakula kwa sababu niliogopa Mungu"

Nehemiah 5:16

pia niliendelea

"Mimi" inahusu Nehemiya.

tulinunua

Neno "sisi" linamaanisha Nehemia na watumishi wake.

watumishi wangu wote walikusanyika

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT 'Nilikusanya watumishi wangu wote huko'

kwa ajili ya kazi

"kufanya kazi kwenye ukuta"

Katika meza yangu walikuwa Wayahudi na maafisa, watu 150, isipokuwa wale waliokuja kwetu kutoka kwa mataifa waliokuwa wakituzunguka.

Nehemia alikuwa na jukumu la kutoa chakula kwa watu wote hawa. Hii inaweza kuelezwa wazi. AT "Pia, kila siku nilikuwa na jukumu la kulisha meza yetu Wayahudi na viongozi, watu 150; na pia tuliwapa wageni waliotoka kutoka nchi nyingine zinazozunguka (UDB)

meza yangu

Hii inahusu meza ya gavana. Ilikuwa meza ya jumuiya kwa jamii na kwa majadiliano ya masuala.

ofisi

"viongozi wa serikali"

Nehemiah 5:18

Taarifa za jumla

(Tazama: tafsili ya namba)

Sasa kilichoandaliwa kila siku kilikuwa

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "Kila siku niliwaambia watumishi wangu kuandaa" au "Kila siku niliwaambia watumishi wangu watutumie nyama kutoka" (UDB)

divai nyingi

"divai ya kutosha kwa kila mtu"

Na hata kwa haya yote sikuhitaji mahitaji ya chakula cha gavana

"lakini sijawahi kuomba malipo ya chakula kwa gavana"

Nikumbuke

Huu ndio idiom. Ni ombi la Mungu kumfikiria na kumkumbuka. AT "Kumbuka mimi"

kwa uzuri

Idiomi hii ni ombi la Mungu kumlipa vitu vyema kwa sababu ya mema ambayo amewafanyia watu. AT "na kulipia mimi" au "kusababisha sababu nzuri kwangu"

Nehemiah 6

Nehemiah 6:1

Sanbalati, Tobia, na Geshemu

Haya ni majina ya wanaume. kama ilivyotafasiriwa katika 2:9

nilijenga ukuta upya... sijawahi

Nehemia alisimamia ujenzi wa ukuta. Yeye hakujenga peke yake. AT "tulijenga ukuta upya ... hatujawahi"

sehemu yoyote

Hii inahusu sehemu ya ukuta. AT "sehemu yoyote ya ukuta kushoto kuvunjwa wazi" au "pengo yoyote katika ukuta wa jiji"

alitumwa kwangu

Hii ina maana kwamba walituma mjumbe na ujumbe. AT "alimtuma mjumbe kwangu"

Ono

Hili ni jina la sehemu.

Nehemiah 6:3

Ninafanya kazi kubwa

Nehemia alikuwa akisimamia ujenzi wa ukuta. Yeye hakujenga mwenyewe. AT 'Mimi ni kusimamia kazi kubwa"

wa nini kazi isimame wakati nitakapoondoka na kuja kwako?

Swali hili la uhuishaji linatumiwa kupinga ombi la Sanballat. Hii inaweza kuandikwa kama taarifa. AT "Siwezi kuruhusu kazi kuacha na kushuka kwako"

chini yako

Neno "chini" linatumika hapa kwa sababu wazi ya Ono ambao walimuomba Nehemia kuja chini ya muinuko kuliko Yerusalemu.

Nehemiah 6:5

Sanbalati alimtuma mtumishi wake kwangu kwa njia ile ile mara ya tano

Sanbalati alimtuma mtumishi wake kwangu kwa njia ile ile mara tano. Kutambua ujumbe huu kwa njia tofauti hutaanisha kuwa ni tofauti kwa njia fulani kutoka kwa ujumbe wa nne uliopita na kwa hiyo, lazima ieleweke.

mara tano

"mara 5"

barua ya wazi

Barua hiyo ilikuwa ni mawasiliano ya kidiplomasia yasiyo wazi. Hii ilikuwa ni matusi kwa mpokeaji kwa sababu barua hiyo ilikuwa huru kusoma na kueneza yaliyomo kati ya watu wa mkoa.

katika mkono wake

Hii inamaanisha kuwa alikuwa na barua katika milki yake, lakini hakuwa na lazima kubeba kwa mkono wake wakati wote. AT "katika milki yake"

Inaripotiwa kati ya mataifa

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT 'Uzoefu katika eneo hilo ni.'

mpango wa kuasi

Hii inamaanisha kuwa wanapinga kuasi dhidi ya mfalme Artaxerxesi mfalme wa Kiajemi, ambaye kwa sasa alikuwa anawanyanyasa Wayahudi. AT "ni mipango ya kuasi dhidi ya Artaxerxesi"

Nehemiah 6:7

Mfalme atasikia

"Mfalme Artaxerxesi atasikia"

Kwa hiyo njoo

"Kwa hiyo njoo na kukutana nasi"

Nehemiah 6:8

Kisha nikatuma maneno kwake

Hapa "mimi" inahusu Nehemia na "yeye" kwa Sanbalati

mambo kama hayo hayajafanyika kama unavyosemaHere Nehemiah requests for God to strengthen him by asking him to strengthen his "hands." AT "strengthen me" or "give me courage"

'"Hakuna mambo ambayo unasema yamefanyika"

kwa maana ndani ya moyo wako umeyabuni

Hapa "moyo" ina maana ya "akili," yaani, tamaa na mawazo ya mtu. AT "kwa ajili ya akili yako uliyabuni" au "kwa kuwa umefanya hivyo katika mawazo yako mwenyewe" (UDB)

Kwa maana wote walitaka kututisha

Hapa "wao" inahusu maadui wa Nehemia, Sanbalati, Tobia, Geshemi, na wafuasi wao. Neno "sisi" linamaanisha Wayahudi.

Wataacha mikono yao kufanya kazi hiyo

Hiya ni maneno ya maana ambayo ina maana kwamba wanaacha kazi yao juu ya ukuta. AT "Wafanyakazi wa ukuta wataacha kufanya kazi"

imarisha mikono yangu

Hapa Nehemia anamuomba Mungu kumtia nguvu kwa kumwomba kuimarisha "mikono yake." AT "kuimarisha" au "nipe ujasiri"

Nehemiah 6:10

Shemaya...Delaya....Mehetabeli

Haya ni majina ya wanaume

ni nani aliyefungiwa nyumbani kwake

Mwandishi haitoi sababu ya kuwa amefungiwa, hivyo ni bora kusema kwamba alikuwa akikaa nyumbani kwa kutumia maneno ya kawaida zaidi iwezekanavyo. AT "ambao mamlaka waliamuru kukaa nyumbani kwake"

Je! Mtu kama mimi ninaweza kukimbia? Na mtu kama mimi ninaweza kuingia hekaluni ili nipate kuishi?

Nehemia anatumia swali hili la kuvutia ili kusisitiza kwamba hatatenda yale Shemaya amesema. Maswali haya yanaweza kuandikwa kama taarifa. AT "Mtu kama mimi siwezi kukimbia. Na mtu kama mimi siwezi kuingia ndani ya hekalu kujificha tu ili aishi hai.

Nehemiah 6:12

lakini alikuwa amefanya unabii

kwa sababu alikuwa ametabilia

na dhambi

Kutumia hekalu kama mahali pa kuficha ilikuwa dhambi. Inaweza kuwa na manufaa kufanya hili wazi. AT "na dhambi kwa kutumia vibaya hekalu

jina baya

Huu ndio idiomi. AT"'ili waweze kunipa sifa mbaya" au "ili waweze kutoa ripoti mbaya juu yangu"

Kumbuka

Huyu ni idiomi. AT: "Kumbuka"

Noadia

Hili ni jina la mwanamke

Nehemiah 6:15

Kwa hiyo ukuta ukamalizika

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "Tumemaliza ukuta"

siku ya ishirini na tano ya mwezi wa Eluli

siku ya tano ya mwezi wa Eluli - "siku 25 ya mwezi wa Eluli." "Eluli" ni mwezi wa sita wa kalenda ya Kiebrania.

siku hamsini -mbili

siku mbilisiku 52

walikata tamaa sana kwa heshima yao wenyewe

"walidhani kidogo sana" au "walipoteza kujiamini"

kazi ilifanyika kwa msaada wa Mungu wetu

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "alikuwa Mungu wetu ambaye alisaidia kukamilisha kazi hii"

Nehemiah 6:17

tuma barua nyingi

Waheshimiwa waliwatuma wajumbe kuleta barua hizi kwa Tobia. AT "aliwatuma wajumbe wengi kwa barua"

Barua za Tobia zilikuja

Hapa barua za Tobia zinajulikana kama kuja kwa wenyewe, wakati zilipoletwa na wajumbe. AT "Tobia alituma barua" au "Tobia aliwatuma wajumbe wengi kwa barua"

Tobia

Tafsiri jina la mtu huyu kama ulivyofanya

ambao walikuwa wamefungwa kwa kiapo kwake

Hii inazungumzia watu kuwa waaminifu kwa Tobia kwa sababu walikuwa wameahidi kiapo kwake kama kwamba kiapo chao kilikuwa kamba kilichofunga miili yao. AT 'aliyemapa kiapo' au 'aliyefanya kiapo na kuwa mwaminifu kwake'

alikuwa mkwe wa Shekania

mkwe wa Shekania - Hii ina maana kwamba Tobia alikuwa amemuoa binti wa Shekania. Tafsiri jina "Shekania' kama ulivyofanya katika 3: 28.

Ara........ Yehohanani

Haya ni majina na watu

Meshulamu ...... Berekia

Haya ni majina ya watu. kama ilivyotafsiliwa 3:3

Pia walizungumza nami kuhusu matendo yake mema na kumwambia maneno yangu

'Waheshimu wa Kiyahudi waliniambia kuhusu matendo mema ya Tobia na kisha nikamwambia kuhusu majibu yangu'

Barua zilitumwa kwangu kutoka kwa Tobia

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. Tobia aliwatuma wajumbe kuleta barua kwa Nehemiya. AT "Tobia alipeleka barua kwangu" au "Tobia aliwatuma wajumbe kuleta barua kwangu"

Nehemiah 7

Nehemiah 7:1

Wakati ukuta ulipomalizika

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "Tulipomaliza ukuta"

milango nimekwisha kuisimamisha,

Hii ilifanywa kwa msaada. AT "Mimi na wengine tulifunga milango"

walinzi wa malango na waimbaji na Walawi walikuwa wamechaguliwa

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. Maana iwezekanavyo ni 1) Nehemiya aliwachagua. AT "Niliwapa walinzi wa mlango na waimbaji na Walawi kwa kazi zao" au 2) Mtu mwingine aliwachagua. AT "waliwapa walinzi wa malango na waimbaji na Walawi kwa kazi zao"

walinzi wa mlango

watu waliopewa kila mlango, wajibu wa kudhibiti upatikanaji wa jiji au hekalu, na kufungua milango na kufungwa mara kwa mara na kwa sababu zilizowekwa na msimamizi

waimbaji

wanamuziki wa sauti ambao waliongoza katika ibada, katika maandamano, na sherehe, na kuzalisha muziki na nyimbo zinazolisisitiza na kuimarisha tukio

Hanani..... Hanania

Haya ni majina ya wanaume.

nikampa ndugu yangu Hanani kuwa na amri

"Nilipa amri ya ndugu yangu Hanani kuwa meneja"

ambaye alikuwa msimamizi wa kijiji

"ambaye alikuwa mkuu wa kjiji"

"kijiji"

"ngome"

alimuogopa Mungu zaidi kuliko wengi

"alimuogopa Mungu zaidi ya watu wengine wengi"

Nehemiah 7:3

Nami nikawaambia

Neno "wao" linamaanisha Hanani na Hananiah.

Msifungue malango ya Yerusalemu mpaka jua litakapokuwa kali. Wakati walinzi wa mlango wanalinda, unaweza kufunga milango na kuikaza

Maana inawezekana ni 1) vitendo hivi vilifanywa na Hanani na Hananiah au 2) vitendo hivi vilifanywa na Hanani na Hananiah kwa msaada wa walinzi wa mlango au 3) walinzi wa mlango walifanya vitendo hivi chini ya uongozi wa Hanani na Hananiah.

jua ni kali

"jua liko juu mbinguni"

Wakati walinzi wa mlango wanalinda, unaweza kufunga milango na kuikaza

"Funga milango na uikaze wakati walinzi wa mlango bado wanalinda"

walinzi wa mlango

Tafsiri hii kama katika 7:1

"Funga milango na kuukaza"

"funga milango na uwafungie"

Chagua walinzi kutoka kwa wale wanaoishi Yerusalemu

"Waagize walinzi kutoka kwa watu hao wanaoishi Yerusalemu"

kituo chao cha ulinzi

"tahadhari" au "nafasi ya ulinzi"

hakuna nyumba zilizojengwa tena

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "watu hawajajenga upya nyumba"

Nehemiah 7:5

weka ndani ya moyo wangu

Hapa "moyo" Nehemia inahusu mawazo na mapenzi yake. Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 2:11. AT "aliongoza mimi" au "aliniongoza"

kuwaandikisha

"kuandika na kujiandikisha"

Kitabu cha kizazi

Hiki kilikuwa kitabu ambacho hakipo tena.

nikaona kwamba imeandikwa humo

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "na kupatikana kuwa mtu ameandika zifuatazo ndani yake"

Nehemiah 7:6

Hawa ndio watu wa jimbo hilo

"Hawa ni wazao wa mkoa huu"

walitoka nje

"walirudi kutoka" au "walirudi kutoka"

walikwenda

Hii ni idiomi ambayo inahusu kusafiri kwenda Yerusalemu, ambayo ilikuwa juu ya ardhi kuliko eneo jirani.

ambao Nebukadreza mfalme wa Babeli aliwachukua mateka

ambaye Nebukadreza, mkuu wa Babeli, aliwaondoa kutoka nchi yao. Jeshi la Babiloni lilifanya hili chini ya amri ya Nebukadreza.

Zerubabeli....... Yoshua...... Nehemia..... Seraya..... Reelaya...... Nahamani...... Mordekai..... Bilshani......Mispari..... Bigwai,.....Rehumu...... Baana

Haya yote ni majina ya wanaume.

Idadi ya wanaume

Sensa ilitolewa wakati Waisraeli waliporudi Yerusalemu baada ya uhamisho. Nambari zinawakilisha jinsi watu wengi walikuwa wa kikundi kila familia. Sentensi hii inaleta habari katika aya zifuatazo.

Nehemiah 7:8

Sentensi unganishi

Nehemia anaelezea idadi ya watu ambao walirudi kutoka uhamishoni. Watu walikusanywa na familia kulingana na jina la baba zao. Nambari inawakilisha idadi ya wanaume katika kila familia.

Paroshi...Shefatia... Ara

Haya ni majina ya wanaume.

Nehemiah 7:11

Sentensi unganishi

Nehemiya anaendelea kuandika idadi ya watu ambao walirudi kutoka uhamishoni.

kwa wana wa Yeshua na Yoabu

"yaani, wana wa Yeshua na Yoabu"

Pahath Moabu...Yeshua ....Yoabu...Elamu....Zatu... Zakai

Haya ni majina ya wanaume.

Nehemiah 7:15

Sentensi unganishi

Nehemiya anaendelea kuandika idadi ya watu ambao walirudi kutoka uhamishoni.

Binnui....Bebai....Azgadi....Adonikamu

Haya ni majina ya wanaume.

Nehemiah 7:19

Sentensi unganishi

Nehemiya anaendelea kuandika idadi ya watu ambao walirudi kutoka uhamishoni.

Bigwai.....Adini...Ateri...Hashumu

Haya ni majina ya wanaume.

Wana wa Ateri, wa Hezekia

Mwandishi amefupisha neno hili. AT "wana wa Ater, ambaye ni wa uzao wa Hezekia"

Nehemiah 7:23

Sentensi unganishi

Nehemiya anaendelea kuandika idadi ya watu ambao walirudi kutoka uhamishoni.

Besai.....Harifu...Gibeoni

Haya ni majina ya wanaume.

Bethlehemu na Netofa

Haya ni majina ya maeneo huko Yuda

Nehemiah 7:27

Sentensi unganishi

Nehemiya anaendelea kuandika idadi ya watu ambao walirudi kutoka uhamishoni.

Anathothi.. Beth Azmaweth... Kiriath Yearimu, Kefira, na Beerothi...Rama na Geba

Haya yote ni majina ya maeneo.

Nehemiah 7:31

Sentensi unganishi

Nehemiya anaendelea kuandika idadi ya watu ambao walirudi kutoka uhamishoni.

Mikmasi...Betheli na Ai...Nebo...Elamu

Haya yote ni majina ya wanaume.

Nehemiah 7:35

Sentensi unganishi

Nehemia anaendelea kuandika idadi ya watu ambao walirudi kutoka uhamishoni.

Harimu...Yeriko...Lodi, Hadidi na Ono...Senaa

Haya yote ni majina ya wanaume.

Nehemiah 7:39

Sentensi unganishi

Nehemia anaendelea kuandika idadi ya watu ambao walirudi kutoka uhamishoni.

Yedaya...Yeshua...Imeri...Pashuri.. Harimu

Haya yote ni majina ya wanaume.

wa nyumba ya Yeshua

Neno "nyumba" ni jina kwa familia. AT "kutoka kwa jamaa ya Yeshua"

Nehemiah 7:43

Sentensi unganishi

Nehemia anaendelea kuandika idadi ya watu ambao walirudi kutoka uhamishoni.

Yeshua...Kadmieli...Binui....Hodavia...Asafu...Shalumu...... Ateri...Talmoni....Akubu...Hatita....Shobai

Haya majina ya wanaume

Waimbaji

Tafsiri hii kama katika 7:1.

walinzi wa mlango

Tafsiri hii kama katika 7:1.

Nehemiah 7:46

Taarifa za jumla

Aya hizi zinaendelea majina ya watu ambao wazao wao walirudi kutoka uhamishoni

Siha...Hasufa...Tabaothi...Kerosi....Siaha...Padoni ...Lebana...Hagaba....Hanani....Gideli...Gahari

Haya ni majina ya wanaume.

Siaha

Huyu ndiye mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Siaha katika Ezra 2:44.

Nehemiah 7:50

Taarifa za jumla

Aya hizi zinaendelea majina ya watu ambao wazao wao walirudi kutoka uhamishoni

Reaya.... Resini.....Nekoda.... Gazamu.... Uza... Pasea... Besai... Meunimu.... Nefusimu

Haya ni majina ya wanaume

Reaya.... Resini.....Nekoda.... Gazamu.... Uza... Pasea... Besai... Meunimu.... Nefusimu

Haya ni majina ya wanaume

Nehemiah 7:53

Taarifa za jumla

Aya hizi zinaendelea majina ya watu ambao wazao wao walirudi kutoka uhamishoni

Bakbuki..... Hakufa.... Harhuri....Baslith...Mehida....Harsha.... Barkosi..... Sisera..... Tema.....Nesia..... Hatifa.

Haya ni majina ya wanaume

Baslith

Hili ni jina la mtu ambaye pia huitwa Bazluti katika Ezra 2:52.

Nehemiah 7:57

Sentensi unganishi

Nehemia anaendelea kuandika idadi ya watu ambao walirudi kutoka uhamishoni.

Sotai...Sofeereth.....Darkoni....Gideli....Shefatia...Hatili.... Pokerethi Sebaimu.... Amoni

Haya ni majina ya wanaume

Sofereti

Hili ni jina la mtu anayeitwa Hasofereti katika Ezra 2:55.

Peruda

Hili ndio jina la mtu ambaye pia huitwa Peruda katika Ezra 2:55.

Nehemiah 7:61

Sentensi unganishi

Nehemia anaendelea kuandika idadi ya watu ambao walirudi kutoka uhamishoni.

akapanda juu

Hii ni idiom ambayo inahusu kusafiri kwenda Yerusalemu, ambayo ilikuwa juu ya ardhi kuliko eneo jirani. AT 'kurudi' au 'kurudi'

Tel Mela...Tel harsha...Kerub....Addon....Imeri

Haya ni majina ya sehemu

Delaya......Tobia..... Nekoda.....Habaya.... Hakosi.... Barzilai

Haya ni majina ya wanaume.

Nehemiah 7:64

Hawa walitafuta rekodi zao kati ya waliojiunga na kizazi chao

"Walitaka kumbukumbu zao za maandishi" au "Walitafuta kumbukumbu zao za maandishi"

Hawa walitafuta

"Hawa" zinamaanisha wana wa Hobaya, Hakozi na Barzilai. (Angalia 7:61)

lakini hawakuweza kuzipata

Hii inaweza kuelezwa kwa fomu ya kazi. AT "lakini hawakuweza kupata rekodi zao"

kwa hivyo waliondolewa katika ukuhani kama walio najisi

Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu ya kazi. Jina la kibinadamu "ukuhani" linaweza kutafsiriwa kama kitenzi 'kazi kama makuhani.' AT "gavana aliwatendea kama walikuwa najisi na hawakuwaruhusu kufanya kazi kama makuhani"

mpaka atakapoinuka kuhani mwenye Urimu na Thumimu.

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "mpaka kuhani aliye naUrimu na Thumimu alikubali"

Urimu na Thumimu.

Haya yalikuwa mawe matakatifu ambayo kuhani mkuu alipitia kifuani pake na kutumika mara kwa mara ili kujua mapenzi ya Mungu.

Nehemiah 7:66

Sentensi unganishi

Nehemia anaendelea kuandika idadi ya watu ambao walirudi kutoka uhamishoni.

Kusanyiko lote kwa pamoja

"Kundi zima pamoja"

ilikuwa 42,360

"ilikuwa watu 42,360"

waimbaji wanaume na wanawake

"waimbaji wanaume na waimbaji wanawake"

Nehemiah 7:68

736 ... 245 ... 435 ... 6,720

Hii ndio idadi ya wanyama waliorejeshwa.

Nehemiah 7:70

wakuu wa familia za baba zao

"mababu wakuu" au "viongozi wa jamaa" (UDB)

waliwapa katika hazina

"kuweka katika hazina"

darkoni elfu moja

"darkoni 1000"

darkoni ya dhahabu

Darkoni ilikuwa sarafu ndogo ya dhahabu ambayo watu wa Dola ya Kiajemi walitumia.

mabakuli

bakuli kubwa

nguo

vitu vya nguo

darkroni elfu ishirini

darkroni 20,000

mane ya fedha

A mane ni karibu nusu ya kilo kwa uzito.

migodi elfu mbili

"migodi 2000"

mavazi sitini

nguo saba - " mavazi 67 "

Nehemiah 7:73

walinzi wa malango

Tafsiri hii kama katika 7: 1.

waimbaji

Tafsiri hii kama katika 7: 1.

baadhi ya watu

Maelezo ya habari ni kwamba hii inahusu baadhi ya Waisraeli ambao hawakuwa makuhani au wafanyakazi wengine wa hekalu.

na Waisraeli wote

Maana iwezekanavyo ni 1) makundi yote ya Waisraeli yaliyoorodheshwa katika aya hii au 2) Waisraeli wengine ambao hawakufanya kazi hekalu.

mwezi saba

"mwezi wa 7." Hii ni mwezi wa saba wa kalenda ya Kiebrania. Ni wakati wa mwisho wa Septemba na sehemu ya kwanza ya Oktoba kwenye kalenda za Magharibi.

wakiishi katika miji yao

"waliishi katika miji yao wenyewe"

Nehemiah 8

Nehemiah 8:1

Watu wote walikusanyika kama mtu mmoja

Hii ni jumuia ambayo inaonyesha watu kwa ujumla wamekusanyika. AT 'Watu walikusanyika pamoja pamoja'

Mlango wa maji

Hili lilikuwa jina la ufunguzi mkubwa au mlango katika ukuta.

Kitabu cha Sheria ya Musa

Hii ingekuwa yote au sehemu ya vitabu vitano vya kwanza vya Agano la Kale.

Siku ya kwanza ya mwezi wa saba

Huu ni mwezi wa saba wa kalenda ya Kiebrania. Siku ya kwanza ya mwezi wa saba ni karibu katikati ya Septemba kwenye kalenda za Magharibi. AT "Siku ya 1 ya mwezi wa 7"

kuleta sheria

"kuleta Kitabu cha Sheria"

wote waliokuwa na uwezo wa kusikia na kuelewa

Hii itajumuisha watoto ambao walikuwa wa umri wa kutosha kuelewa kilichosomwa.

alisoma kutoka kwake

Hapa "kwake" ina maana ya Kitabu cha Sheria ya Musa.

Nehemiah 8:4

Matithia, Shema, Anaya, Uria, Hilkia na Maaseya...Pedaya, Misbaeli, Malkiya, Hashumu, Hashbadani, Zekaria na Meshulamu

Haya yote ni majina ya wanaume.

Ezra alifungua kitabu mbele ya watu wote

Neno hili "mbele" linaweza kutafsiriwa kwa kitenzi "tazama." AT "Kila mtu aliona Ezra kufungua kitabu"

kitaba

"Kitabu cha sheria"

alikuwa amesimama juu ya watu

"alikuwa amesimama juu kuliko watu"

alipoufungua watu wote wakasimama.

Watu wakasimama kwa heshima ya neno la Mungu.

Nehemiah 8:6

Ezra akamshukuru Bwana

Jina hili "shukran" linaweza kutafsiriwa kama kitenzi. AT "Ezra alishukuru Bwana"

Yeshua, Bani, Sherebia, Yamini, Akubu, Shabethai, Hodai, Maaseya, Kelita, Azaria, Yozabidi, Hanania, Pelaya nao ni Walawi, waliwasaidia watu kuelewa sheria,

Haya yote ni majina ya wanaume

wakaeleza wazi kwa tafsiri na kutoa maana

Ufafanuzi wa maneno "tafsiri" na "maana" yanaweza kutafsiriwa kama vitenzi. AT "akifafanua wazi na kuelezea"

yaliyosomwa

"nini kilichosomwa"

Nehemiah 8:9

Kwa watu wote walilia

Hiki ni kizazi ambayo inaonyesha kulikuwa na kilio kikubwa kati ya watu. AT "Kwa watu walilia sana"

mule vilivyonona na kunywa kilicho kizuri

Maelezo ya habari ni kwamba watu waliambiwa kula chakula cha kizuri na vinywaji vyema. AT "kula chakula tajiri na kunywa kitu tamu"

Msiwe na huzuni

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "usiwe na huzuni"

kwa kuwa furaha ya Bwana ni nguvu zenu

Majina haya "furaha" na 'nguvu' yanaweza kutajwa kama vitenzi au vigezo. 'Kushangilia kwa Bwana kutakukinga' au 'kufurahi katika Bwana itakuwa kikao chako cha kukimbilia'

Nehemiah 8:11

Nyamazeni

"Nyamaza!' au 'kimya!"

Msiwe na huzuni

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "usiwe na huzuni"

sherehekea kwa furaha kubwa

mantiki ya neno "furaha linaweza kutajwa kama kitenzi. AT "kufurahi sana"

maneno yaliyojulikana kwao

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "maneno ambayo aliwaambia"

Nehemiah 8:13

Siku ya pili

"Siku ya 2 "au" Siku ya pili "

ili kupata ufahamu kutoka

Maana nyingine ya neno "ufahamu" linaweza kutajwa kama kitenzi. AT "kuelewa"

mwezi wa saba

"mwezi wa 7." Huu ni mwezi wa saba wa kalenda ya Kiebrania. Ni wakati wa mwisho wa Septemba na sehemu ya kwanza ya Oktoba kwenye kalenda za Magharibi.

Wanapaswa kutoa tamko

"Wanapaswa kutangaza"

mhadsi

aina ya mti mdogo wenye maua yenye rangi

miti ya kivuli

"miti ya majani"

kufanya mavazi ya muda

"kufanya hema"

kama ilivyoandikwa

Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu ya kazi. AT "kama Musa alivyoandika kuhusu hilo"

Nehemiah 8:16

wakajifanyia mahema

"walijenga hema zao wenyewe"

lango la Maji.... lango la Efraimu

Haya ni majina ya fursa kubwa au mlango katika ukuta.

katika mraba wa lango la Efraimu

"mahali pa wazi na lango la Efraimu"

tangu siku za Yoshua

"Kuanzia siku za Yoshua"

mwana wa Nuni

"Nuni" ni jina la kiume

furaha ilikuwa kubwa sana.

Jina hili "furaha" linaweza kutajwa kama kivumbuzi. AT "watu walifurahi sana"

Nehemiah 8:18

siku kwa siku

"kila siku"

kuanzia siku ya kwanza hadi ya mwisho

Maelezo ya habari ni kwamba ilikuwa wakati wa wiki nzima ya tamasha hilo. AT "kutoka siku ya kwanza hadi siku ya mwisho ya juma"

Walifanya tamasha

'"Walifanya sikukuu" au "Walisherehekea tamasha"

siku ya nane

"siku 8"

kusanyiko zuri

Huu ulikuwa mkutano maalum wa dini.

kwa utiifu wa amri

Taarifa iliyotarajiwa ni kwamba "amri" ilikuwa amri ya Bwana kuhusu jinsi tamasha la nyumba lilivyokuwa limeisha. AT "kama Mungu alivyoamuru"

Nehemiah 9

Nehemiah 9:1

Siku ishirini na nne ya mwezi huo huo

siku ya nne ya mwezi huo huo - "siku ya ishirini na nne ya mwezi wa saba' Hii iko karibu katikati ya Oktoba kwenye kalenda za Magharibi

watu wa Israeli walikusanyika

"'watu wa Israeli walikusanyika"

walikuwa wamevaa magunia, nao wakaweka vumbi juu ya vichwa vyao

Ilikuwa ili kuonyesha jinsi walivyokuwa na huruma kwa mambo mabaya wao na baba zao waliyofanya.

Wazao wa Israeli

Waisraeli

walijitenga na wageni wote

"hakuwa na kitu chochote cha kufanya na wale ambao hawakuwa Waisraeli"

Walisimama na kukiri dhambi zao wenyewe na matendo maovu ya baba zao

"Walikubali mambo mabaya waliyoyafanya na pia mambo mabaya ambayo baba zao walifanya"

Nehemiah 9:3

Wakasimama

Waisraeli wote wakasimama

walikuwa wakikiri

"walikuwa wanakubali mambo mabaya waliyofanya"

na kuinama mbele

"kuabudu" au " kumsifu"

Walawi, Yeshua, Bani....walisimama juu ya ngazi

Matoleo mengine yanatafsiri, "Yeshua, Bani ... alisimama juu ya ngazi zilizojengwa kwa Walawi"

Yeshua, Bani, Kadmieli, Shebaniya, Buni, Sherebia, Bani na Kenani

majina ya wanaume

Nehemiah 9:5

Ndipo Walawi...akasema, "Simameni...milele"

Hapa Walawi wanazungumza na watu wa Israeli.

mkamsifu Bwana

"kumbariki Bwana"

Yeshua....... Kadmieli....... Bani,......Hashabneya, ..... Sherebia

majina ya wanaume. Tafsiri katika 9:3.

Hashabneya.....Hodia.....Pethalia

majina ya wanaume

Libarikiwe jina lako tukufu

alawi wanazungumza na Bwana. "Watu wa Yuda walibariki jina lako tukufu, Bwana"

mbingu za juu, na jeshi lake lote ... jeshi la mbinguni likuabudu wewe

Mwenyeji ni jeshi. "Majeshi ya mbinguni" anasema kwa mfano wa nyota nyingi kama kwamba walikuwa jeshi. Nyota kwa upande wake ni mfano wa malaika wengi. Nyota zinaomwabudu Bwana ni mfano wa malaika wanaomwabudu Bwana. (UDB)

Nehemiah 9:7

Sentensi Unganishi

Katika aya hizi, Walawi wanaendelea kumsifu Bwana mbele ya watu wa Israeli.

Uri wa Wakaldayo

"Uri, ambapo kundi la Wakaldayo liliishi"

Uliona moyo wake ulikuwa mkamilifu mbele yako

Moyo, ndani ya mtu, inawakilisha mtu. AT "Uliona kwamba alikuwa mwaminifu kabisa kwako"

Wakanaani..... Mhiti...... Mwamori..... Perizi......Myebusi.......Wagirgashi

majina ya kundi la watu

Nehemiah 9:9

Sentensi Unganishi

Katika aya hizi, Walawi wanaendelea kumsifu Bwana mbele ya watu wa Israeli.

Uliona

Bwana aliona

umesikia kilio chao

Maelezo ya taarifa ni kwamba Mungu alisogeza hatua kwa sababu kilio cha Waisraeli wakiomba msaada.

ishara na maajabu juu ya Farao

Vifo vilijaribu moyo wa Farao, na wakawa mashahidi dhidi ya ugumu wa moyo wake . AT "ishara na maajabu yaliyothibitisha dhidi ya Farao" au "ishara na maajabu yaliyomhukumu Farao"

watu wote wa nchi yake

"Wamisri wote"

walifanya kwa kujivunia dhidi yao

"walikuwa wenye kiburi juu ya Waisraeli "au" aliwadhulumu wateule wa Mungu

ulijifanyia jina kwa ajiri yako mwenyewe

Hii ni njia nyingine ya kusema "ulionyesha dunia tabia yako" au "ulionyesha uwezo wako."

ambalo linasimama hadi siku leo.

"ambalo watu bado wanalikumbuka"

Nehemiah 9:11

Sentensi unganishi

Katika aya hizi, Walawi wanaendelea kumsifu Bwana mbele ya watu wa Israeli.

umegawanya bahari

Mungu aligawanywa

wewe ... wale waliokuwa wakiwafuata ukawatupa ndani ya kilindi, kama jiwe ndani ya maji ya kina

Katika mfano huu, mwandishi huelezea Mungu akitupa Wamisri ndani ya bahari kwa urahisi kama mtu atakayepiga jiwe ndani ya maji, na jiwe litatoweka chini ya maji kabisa.

Nehemiah 9:12

Sentensi unganishi

Katika aya hizi, Walawi wanaendelea kumsifu Bwana mbele ya watu wa Israeli.

Umewaongozas

Bwana aliwaongoza Waisraeli.

umeshuka

Wakati Mungu akizungumza na watu wake, mara nyingi anaelezewa kama "kushuka" au "kushuka kutoka mbinguni." Hii ni njia ya kueleza kwamba Mungu alionekana kwa mtu huyo. AT "ulionekana" au" umeshuka kutoka mbinguni"

amri za haki na sheria za kweli, amri nzuri na maagizo

Maneno haya mawili yanaelezea kitu kimoja, sheria ya Musa

Nehemiah 9:14

Sentensi unganishi

Katika aya hizi, Walawi wanaendelea kumsifu Bwana mbele ya watu wa Israeli.

amri..... maagizo...... sheria

Kila moja ya maneno haya matatu yanahusu sheria ya Musa.

Nehemiah 9:16

Sentensi unganishi

Katika aya hizi, Walawi wanaendelea kumsifu Bwana mbele ya watu wa Israeli.

wao na baba zetu

Waisraeli wakati wa Musa na watu wa Israeli baada ya wakati wa Musa

wao walikuwa wakaidi ... wakawa wakaidi

Maneno halisi ni "walifanya ngumu zao ngumu." Ikiwa lugha yako ina dalili tofauti ya kuwa mkaidi, ungependa kuitumia hapa.

maajabu uliyofanya kati yao

"miujiza uliyoifanya kati yao"

wakamchagua kiongozi wairudie hali ya utumwa

"walimteua kiongozi kuwapeleka kwenye nchi waliyokuwa watumwa."

ambaye amejaa msamaha

Nia ya kusamehe inazungumzwa kama kama ni maji ambayo inaweza kujaza chombo. AT "ambaye yupo tayari kusamehe"

wingi katika upendo thabiti

Upendo umesemekana kama ni mazao ya chakula ambayo Bwana angeweza kushirikiana na watu. AT "anapenda watu wake sana"

Nehemiah 9:18

Sentensi unganishi

Katika aya hizi, Walawi wanaendelea kumsifu Bwana mbele ya watu wa Israeli.

wewe.... haukuwaacha

Bwana hakuwaacha Waisraeli.

kutupa ndama kutokana na chuma kilichochombwa

chuma kilichochomwa na kuumbwa kwa sura ya ndama

Nguzo ya wingu .... nguzo ya moto

Tafsiri katika 9:12.

Nehemiah 9:20

Sentensi unganishi

Katika aya hizi, Walawi wanaendelea kumsifu Bwana mbele ya watu wa Israeli.

Roho wako mzuri....mana yako... maji

Mwandishi hubadili neno la kawaida ili kusisitiza mambo mema ambayo Bwana aliwapa watu wake. Lugha yako inaweza kuwa na njia nyingine ya kusisitiza vitu hivi.

fundisha

"fundisha"

mana yako haukuwanyima kinywani mwao

Litotesi hii inaweza kuelezewa vizuri. AT "na wewe kwa upole uliwapa mana"

kinywani mwao

Kinywa ni busara kwa mtu mzima. AT kutoka kwao

Nehemiah 9:22

Sentensi unganishi

Katika aya hizi, Walawi wanaendelea kumsifu Bwana mbele ya watu wa Israeli.

Uliwapa falme

Bwana akawapa Waisraeli falme .

Uliwapa falme na watu

"aliwawezesha kushinda falme na watu"

ukawapa kila kona ya nchi

"kuwawezesha kumiliki kila sehemu ya ardhi"

Sihoni .....Ogu

Haya ni majina ya wafalme.

Heshboni....Bashani

Haya ni majina ya maeneo.

Nehemiah 9:23

Sentensi unganishi

Katika aya hizi, Walawi wanaendelea kumsifu Bwana mbele ya watu wa Israeli.

Uliwafanya watoto wao

Bwana aliwafanya wana wa Israeli wakati wa Musa

Ukawatia mikononi mwao

Wakanaani wanasemwa kama walikuwa vitu vidogo ambavyo mtu anaweza kuweka mkononi mwa mtu mwingine. Kutoa kitu ndani ya mkono wa mtu ni kumpa mtu huyo udhibiti kamili juu ya jambo hilo. AT "imewezesha Waisraeli kuwa na udhibiti kamili juu yao"

Nehemiah 9:25

Sentensi unganishi

Katika aya hizi, Walawi wanaendelea kumsifu Bwana mbele ya watu wa Israeli.

Wao waliteka

Waisraeli wakati wa Musa waliteka

nchi yenye ustawi

"ardhi yenye rutuba"

birika zilizochimbwa

mashimo katika ardhi ambapo watu kuhifadhi maji

wakatosheka

Hii inaweza kuwa mfano kwa "kuacha kufikiri kuhusu Bwana "au" wakawa hasira"

Nehemiah 9:26

Sentensi unganishi

Katika aya hizi, Walawi wanaendelea kumsifu Bwana mbele ya watu wa Israeli.

Walitupa sheria yako nyuma ya migongo yao

Sheria inasemekana kama ni kitu ambacho hakina maana ambacho mtu anaweza kutupa. AT "Walichukulia sheria yako haikuwa na maana na hawakujali"

Walitupa sheria yako

Waisraeli walitupa sheria ya Bwana.

hiyo ukawatia mikononi mwa adui zao

Hapa neno "mkono" (sehemu) linaashiria uwezo wa "maadui" (kama watu wote) kufanya madhara. AT "umeruhusu maadui wa watu wako kuwadhuru watu wako"

uliwatuma waokoaji waliowaokoa katika mikono ya adui zao

Hapa neno "mkono" (sehemu) linaashiria uwezo wa "maadui" (kama watu wote) kufanya madhara. AT "uliwatuma watu kuacha adui zao kuwadhuru"

Nehemiah 9:28

Sentensi unganishi

Katika aya hizi, Walawi wanaendelea kumsifu Bwana mbele ya watu wa Israeli.

walipumzika, wakafanya mabaya tena mbele yako

Hapa "wao" inawakilisha Waisraeli na "wewe" kwa Bwana.

ukawaacha mikononi mwa adui zao

Hapa neno "mkono" (sehemu) linaashiria "adui" (kwa ujumla) kufanya madhara. AT "umeruhusu adui zao kuwadhuru"

hawakusikiliza amri zako

Ikiwa lugha yako ina neno la "sikiliza" ambayo pia inamaanisha "utii," tumia hapa.

amri zako ambazo huwapa uzima mtu yeyote anayewatii

Bwana mwenyewe anasemwa kama kwamba yeye alikuwa na amri wenyewe. AT "hata kama wewe huwapa uzima kila mtu anayeitii amri zako"

Nehemiah 9:30

Sentensi unganishi

Katika aya hizi, Walawi wanaendelea kumsifu Bwana mbele ya watu wa Israeli.

Kwa hiyo ukawatia mikononi mwa watu wa jirani

Hapa neno "mkono" (sehemu) linaashiria uwezo wa "watu wa jirani" (kama watu wote) kufanya madhara. AT "umeruhusu watu wa jirani kuwaumiza watu wako" Maneno sawa yanaonekana katika 9:26.

umetoa

Bwana ametoa

haukufanya mwisho wao kabisa

"hauku waaangamiza"

Nehemiah 9:32

Sentensi unganishi

Katika aya hizi, Walawi wanaendelea kumsifu Bwana mbele ya watu wa Israeli.

usiruhusu shida hii yote iwe ndogo kwako ambayo imetujia ... hata leo

Inawezekana kugawanya hii katika sentensi mbili. "Usiruhusu shida hii yote iwe ndogo kwako. Tatizo limekuja kwetu ... hata leo"

shida ... imetujia ...yote yaliyotupata

Maneno "kuja juu yetu" yanazungumzia mambo mabaya yanayotokea kama kwamba ni watu wanaosababisha. AT "madhara ... tumesikia ... kila kitu tumeteseka"

Nehemiah 9:35

Sentensi unganishi

Katika aya hizi, Walawi wanaendelea kumsifu Bwana mbele ya watu wa Israeli.

wakati walifurahia wema wako kwao

"wakati walifurahia mambo mema uliyowapa"

hawakukutumikia

"hawakuitii sheria yako au mafundisho"

Nehemiah 9:36

Sentensi unganishi

Katika aya hizi, Walawi wanaendelea kumsifu Bwana mbele ya watu wa Israeli.

zawadi zake nzuri

"mambo yote mema ndani yake" au "vitu vyote vyema tunaweza kupata kutoka kwake"

Mavuno mazuri kutoka nchi yetu huenda kwa wafalme

"Tunatoa kodi kwa wafalme kwa kufanya kazi nchi yetu"

Wanatawala.

Wafalme mtawala.

Nehemiah 9:38

Sentensi unganishi

Katika aya hizi, Walawi wanaendelea kumsifu Bwana mbele ya watu wa Israeli.

Kwa sababu ya yote haya

kwa sababu watu hawakuitii na Bwana alikuwa amewaadhibu

Kwenye hati iliyofungwa ni majina

Msomaji anapaswa kuelewa kwamba wanaume waliandika majina yao kwenye hati kabla ya kufungwa

Nehemiah 10

Nehemiah 10:1

Katika nyaraka zilizofunikwa walikuwa

Unaweza kuhitaji kujaza maneno yasiyopo. "Katika nyaraka zilizofunikwa zilikuwa majina ya watu wafuatayo"

nyaraka zilizofunikwa

Nyaraka zimefunikwa baada ya majina kusainiwa kwenye nyaraka.

Nehemia

Watu wengine wanaamini kwamba Nehemia aliandika kitabu hiki (angalia UDB) na anajisema mwenyewe kama yeye ni mtu mwingine kwa sababu hii ni orodha rasmi.

Hakalia

Hili ni jina la mtu. Tafsiri katika 1: 1.

Sedekia, Seraya......Yeremia, Pashuri, Amaria

Haya ni majina ya wanaume

Azaria

Hili ni jina la mtu. Tafsiri katika 3:22.

Malkiya

Hili ni jina la mtu. Tafsiri katika 3:11.

Nehemiah 10:4

Taarifa za jumla

Katika aya hizi, Nehemia anaweka majina ya makuhani waliosaini waraka uliofunikwa. (Tazama 10:1)

Hamshi

Hili ni jina la mtu. Tafsiri kama kwa 3 8.

Shekania.......Meshulamu

Hizi ni majina ya wanaume. Tafsiri katika 9:3

Maluki......Obadia, Danieli, Ginethoni...Abiya, Miyamini, 8Maazia, Bilgai

Haya ni majina ya wanaume

Harimu

Hili ni jina la mtu. Tafsiri kama kwa 3:11.

Meremothi

Hili ni jina la mtu. Tafsiri kama kwa 3:3.

Baruki

Hili ni jina la mtu. Tafsiri kama kwa 3:20

Shemaya

Hili ni jina la mtu. Tafsiri katika 3 :28.

Hawa walikuwa makuhani.

Hii inahusu orodha ya awali ya wanaume walio saini waraka. AT "Haya ndio majina ya makuhani waliosaini hati"

Nehemiah 10:9

Taarifa za jumla

Katika aya hizi, Nehemia anaendelea kuandika majina ya watu walio saini hati iliyofunikwa.

Walawi walikuwa

Hii inahusu wale wanaweka majina yao kwenye nyaraka zilizofunikwa. AT "Walawi ambao waliweka majina yao kwenye nyaraka zilizofunikwa"

Yeshua...Henadadi

Haya ni majina ya wanaume. Tafsiri kama 3:18.

Azania.... Rehobu...Beninu

Haya ni majina ya wanaume.

Binui

Hili ni jina la mwanaume. kama ilivyo tafasiliwa katika 3:22

Kadmieli

Hili ni jina la mwanaume. kama ilivyo tafasiliwa katika 7:43

Shebania

Hili ni jina la mwanaume. kama ilivyo tafasiliwa katika 9:3.

Hodia.....Kelita.....Pelaya.....Sherebia

Haya ni majina ya wanaume . kama ilivyo tafasiliwa 8:6

Hanani

Hili ni jina la mwanaume. kama ilivyo tafasiliwa katika 7:46

Mika

Hili ni jina la mwanaume. kama ilivyo tafasiliwa katika 10:9.

Hashabia.....Bani

Haya ni majina ya wanaume. Tafsiri kama 3:16

Zakuri

Hili ni jina la mwanaume. kama ilivyo tafasiliwa katika 3:1

Viongozi wa watu walikuwa

Hii inahusu wale wanaweka majina yao kwenye nyaraka zilizofunikwa. AT "Viongozi wa watu ambao waliweka majina yao kwenye nyaraka zilizofunikwa walikuwa"

Paroshi

Hili ni jina la mwanaume. kama ilivyo tafasiliwa katika 3:25.

Pahath-Moabu

Hili ni jina la mwanaume. kama ilivyo tafasiliwa katika 3:11

Elamu.........Zatu

Hili ni jina la mwanaume. kama ilivyo tafasiliwa katika7:11

Nehemiah 10:15

Taarifa za jumla

Katika aya hizi, Nehemia anaendelea kuandika majina ya watu walio saini hati iliyofunikwa.

Buni

Hili ni jina la mtu. kama ilivyo tafsiri katika 9:3.

Azgadi, Bebai

Haya ni majina ya wanaume. kama ilivyo tafsiriwa katika 7:15.

Adoniya....Azuri....Nobai......Magpiashi....Heziri....Yadua

Haya ni majina ya wanaume.

Bigwai

Hili ni jina la mtu. kama ilivyo tafsiri katika 7:6

Adini, Ateri, Hezekia......Hashumu

Haya ni majina ya wanaume. kama ilivyo tafsiriwa katika 7:19

Hodia

Hili ni jina la mtu. kama ilivyo tafsiri katika 8:6

Besai, Harifu

Haya ni majina ya wanaume. kama ilivyo tafsiriwa katika 7:23

Anathothi

Huli ni jina la mwanaume. kama ilovyo tafsiriwa katika 7:27

Meshulamu....Meshezabeli, Sadoki

Haya ni majina ya wanaume. kama ilivyo tafsiriwa katika 3:3

Nehemiah 10:22

Taarifa za jumla

Katika aya hizi, Nehemia anaendelea kuandika majina ya watu walio saini hati iliyofunikwa.

Pelatia...Hoshea....Pilha, Shobeki....Hashabna...Ahia.... Anani.... Harimu..... Baana.

Haya ni majina ya wanaume .

Hanani

Hili mi jina la mwanaume. kama ilivyo tafsriwa katika 7:46

Hanania

Hili mi jina la mwanaume. kama ilivyo tafsriwa katika 8:4

Hanania

Hili ni jina la mwanaume. kama ilivyo tafsriwa katika 3:8

Hashubu.....Haloheshi

Haya ni majina ya wanaume. kama ilivyo tafsiriwa katika 3:11

Rehumu

Hili ni jina la mwanaume. kama ilivyo tafsriwa katika 3:16.

Maaseya

Hili ni jina la mwanaume. kama ilivyo tafsriwa katika 3:22.

Maluki, Harimu

Haya ni majina ya wanaume. Kama ilivyo tafsriwa katika 10:4

Baana

Hili ni jina la mwanaume. Kama ilivyo tafsriwa katika 7:6.

Nehemiah 10:28

walinzi wa malango

Hii inawakilisha watu waliopewa kila mlango, wajibu wa kudhibiti upatikanaji wa jiji au hekalu, na kufungua na kufunga milango kwa wakati na kwa sababu zilizowekwa na msimamizi. Tazama jinsi ilivyotafasiri hii katika 7 1.

waimbaji

"waimbaji wa hekalu"

wote walio na ujuzi na ufahamu

Maneno haya yanaweza kuwekwa wazi. AT "wote ambao walikuwa wazee wa kutosha kuelewa kile kilichoahidi kumtii Mungu maana yake"

ndugu zao, wakuu wao

"ndugu zao ambao ni wakuu" au "ndugu zao ambao ni viongozi." Maneno haya yanataja watu sawa.

kujifunga katika laana na kiapo

Hii inazungumzia watu wanaoapa na laana kama kwamba kiapo na laana zilikuwa kamba ambayo iliwafunga kimwili. 'Waliapa kwa kiapo na laana' au 'waliapa na wakaita laana ya kuja wenyewe ikiwa hawakuiweka'

kutembea katika sheria ya Mungu

Hii ndio idiomi. AT "kuishi kwa sheria ya Mungu" au "kutii sheria ya Mungu"

iliyotolewa na Musa mtumishi wa Mungu

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "ambayo Musa mtumishi wa Mungu alikuwa amewapa Israeli"

kuzingatia

"kufuata"

Nehemiah 10:30

Taarifa za Jumla

Katika aya hizi, watu wanaelezea maudhui ya kiapo waliyoifanya katika 28:28.

hatuwezi kuwapa binti zetu watu wa nchi au kuchukua binti zao kwa wana wetu

Hii ina maana kwamba hawataruhusu wana na binti zao kuolewa nao. AT "haiwezi kuwapa binti zetu kuoa watu wa nchi au kuchukua binti zao kuoa zetu"

watu wa nchi

Hii inawakilisha watu wanaoishi katika nchi yao ambao hawaabudu Bwana. AT "watu wa nchi hii ambao hawaabudu Bwana"

Tuliahidi ... hatuwezi kutoa ... hatuwezi kununua ... tutaacha ... tutafuta

Neno "sisi" hapa ni pamoja na Nehemia na watu wa Kiyahudi, lakini si msomaji wa kitabu hiki."

mwaka wa saba

"Mwaka wa 7"

utaacha mashamba yetu kupumzika

Huu ndio idiomi. AT "hatuwezi kulima mashamba yetu" au "hatuwezi kukua chochote katika mashamba yetu"

tutafuta madeni yote yaliyotokana na Wayahudi wengine

"tutafuta madeni yote kwa Wayahudi wengine" au "tutawasamehe madeni yote inayomilikiwa na Wayahudi wengine"

Nehemiah 10:32

Taarifa ya Jumla

Katika aya hizi, watu wanaendelea kuelezea yaliyomo ya kiapo waliyoifanya

Tulikubali amri

'Tuliahidi kumtii amri

Tulikubali

Neno "sisi" hapa inajumuisha Waisraeli wote ikiwa ni pamoja na Nehemiya isipokuwa kwa kuhani na Walawi, na sio pamoja na msomaji wa kitabu hiki

shilingi ya shekeli

"1/3 ya shekeli." "Ya tatu" ina maana sehemu moja kati ya sehemu tatu sawa. Hii inaweza kuandikwa kwa vipimo vya kisasa. AT "5 gramu ya shaba"

ajili ya huduma ya

"kulipa huduma ya"

mkate wa uwepo

Hii inahusu mikate 12 ya mikate iliyotiwa bila yachu iliyohifadhiwa katika hekalu na kutumika kutumikia kuwepo kwa Mungu na watu wake.

sikukuu mpya za mwezi

Hizi ndizo maadhimisho yaliyofanyika wakati mwezi ulikuwa na muonekao mdogo mbinguni.

Nehemiah 10:34

Taarifa ya Jumla

Katika aya hizi, watu wanaendelea kuelezea yaliyomo ya kiapo waliyoifanya 10:28

kuteketezwa

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "kwa ajili ya Walawi kuwaka"

kama ilivyoandikwa

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "kama isemavyo"

kutoka kwenye udongo wetu

"katika udongo wetu" au "juu ya ardhi yetu"

Nehemiah 10:37

Taarifa ya Jumla

Katika aya hizi, watu wanaendelea kuelezea yaliyomo ya kiapo waliyoifanya

Tutaleta ... Tutaleta

Neno "sisi" hapa ni pamoja na Nehemia na Waisraeli isipokuwa kwa makuhani na Walawi, na pia hajumuishi msomaji wa kitabu hiki

unga wa kwanza

Unga ni "unga mzima" au "nafaka ya ardhi."

na divai mpya na mafuta

Maneno ya kukosa yanaweza kuongezwa. AT "na ya kwanza ya divai mpya na mafuta" au "na bora ya divai mpya na mafuta"

vyumba vya kuhifadhi vya nyumba ya Mungu wetu

"mahali ambapo vitu vilihifadhiwa katika hekalu"

zaka kutoka kwenye ardhi yetu

Hapa "udongo wetu" inahusu kila kitu kilichopandwa chini. AT "ya kumi ya kile tunachokua chini"

wanapokea zaka

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "watu huwapa zaka"

sehemu ya kumi

Hii ina maana sehemu moja kati ya kumi iliyosawa

vyumba vya kuhifadhi hazima

vyumba vya kuhifadhi katika hekalu

Nehemiah 10:39

Taarifa za Jumla

Katika aya hizi, watu kumaliza kuelezea yaliyomo katika kiapo walichofanya

katika vyumba vya kuhifadhi ambapo vitu vya patakatifu vinasimamishwa

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. Kwenye "vyumba ambapo makuhani huweka vitu vilivyotumiwa katika hekalu"

Hatuwezi kuacha nyumba ya Mungu wetu

Hii inaweza kuelezwa kwa fomu nzuri. AT "Tunatunza kwa ajiri ya hekalu"

Tutakuwa

Neno "sisi" hapa ni pamoja na Nehemia na watu wote wa Israeli lakini haijumuishi msomaji wa kitabu hiki

Nehemiah 11

Nehemiah 11:1

watu walipiga kura

"watu walitupa mawe ya alama ili kuamua ni nani atakayehusika"

kuleta moja kati ya kumi

"kuleta familia moja kutoka kila familia kumi"

Nehemiah 11:3

katika nchi yake mwenyewe, ikiwa ni pamoja na Waisraeli

"katika nchi yake Israeli Waisraeli"

baadhi ya wana wa Yuda na baadhi ya wana wa Benyamini

"baadhi ya watu wa Yuda na baadhi ya watu wa Benyamini"

Watu kutoka Yuda walijumuishwa

"Kutoka kwa wana wa Yuda"

Benyamini.......Athaya......Uzia......Zekaria..... Amaria......Shefatia.......Mahalaleli......Peresi

Haya ni majina ya wanaume.

wazao wa Perez

"kutoka kwa wazao wa Perezi"

Nehemiah 11:5

Sentensi Unganishi

Katika aya hizi, Nehemia anaendelea kuandika maafisa wa mkoa ambao waliishi Yerusalemu

Maaseya..... Baruki......Kolhoze.......Hazaya......Adaya....... Yoyaribu.....Zakaria....Peresi

Haya ni majina ya wanaume.

Baruki

mtu kutoka mji wa Shilo

wana wa Perezi

"wazawa wa Peresi"

468. Walikuwa masujaa.

"468 wanaume mashujaa" au "468 wanaume wenye ujasiri"

Nehemiah 11:7

Sentensi Unganishi

Katika aya hizi, Nehemia anaendelea kuandika maafisa wa mkoa ambao waliishi Yerusalemu

Benyamini.......Salu......Meshulamu......mwana .....Yoedi......Pedaya......Kolaya.....Maaseva..... Ithiel......Yehaya......Gabai......Salai....Yoeli .....Zikri......Yuda......Hasenua

Haya ni majina ya wanaume.

Nehemiah 11:10

Yedaya.....Yoyaribu.....Yakini......Seraya ....Hilikia.......Meshulamu......Sadoki.....Merayoti, .....Ahitubu.....Adaya......Yerohamu......Pelalia...... Amzi....Zekaria, .....Pashuri......Malkiya

Haya ni majina ya wanaume.

waliofanya kazi ya ukoo

"Nyumba" ni "nyumba ya Mungu" (11:11). "ambaye alifanya kazi hekaluni"

washirika wao

"ndugu zao" au "jamaa zao"

Nehemiah 11:13

Ndugu zake

ndugu za Adaya, mwana wa Jerohamu (11"10).

ndugu

Neno hili ni mfano kwa 1) Waisraeli wenzake au 2) watu ambao walifanya kazi hiyo hiyo. AT "washirika" au "wafanyakazi wenzake"

Maasai ........Azareli.....Azai, .....Meshilemothi, .....Imeri.....Zabdieli....Hageoli.

Haya ni majina ya wanaume.

wapiganaji wenye ujasiri

"wapiganaji mashujaa" au "mashujaa wa ujasiri"

Nehemiah 11:15

Shemaya...Hashubu....Azrikamu...Hashabia.....Buni, ..... Shabethai....Yozabadi

Haya ni majina ya wanaume

ambao walikuwa ni viongozi wa Walawi, waliosimamia

"kutoka kwa viongozi wa Walawi, walikuwa wasimamizi"

Nehemiah 11:17

Matania....Mika...Zakri....Bakbukia......Abda.... Shemaya....Galali....Yeduthuni

Haya ni majina ya wanaume.

aliyeanza shukrani kwa sala

Hiyo ni nani aliyeongoza waimbaji (angalia UDB).

Bakbukia, wa pili miongoni mwa ndugu zake

Maana iwezekanavyo ni 1) Bakbukia alikuwa jamaa wa Matania na pili alikuwa na mamlaka kwa Matania (angalia UDB) au 2) "Bakbukia aliongoza kundi la pili la waimbaji."

ndugu

Njia nyingine inayowezekana ni "washirika" au "wafanyakazi wenzake" (tazama UDB).

mji mtakatifu

Maneno haya yanamaanisha mji wa Yerusalemu.

Nehemiah 11:19

walinzi wa malango

watu waliopewa kila mlango, wajibu wa kudhibiti upatikanaji wa jiji au hekalu, na kufungua na kufunga milango kwa nyakati na kwa sababu zilizowekwa na msimamizi. Tafsiri kama katika 7:1.

Akubu....Talmoni.....Siha.....Gishpa

Haya ni majina ya wanaume

Ofeli

Hili ni jina la eneo.

Nehemiah 11:22

Mtawala mkuu

"Mwangalizi"

Uzi....Bani...Hashabia.... Matania....Mika....Asafu...Pethahia....Meshezabeli.... Zera.....Yuda

Haya ni majina ya wanaume.

Walikuwa chini ya maagizo kutoka kwa mfalme

"Mfalme alikuwa amewaambia nini cha kufanya"

maagizo imara yalitolewa kwa waimbaji

Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu ya kazi. AT "mfalme alikuwa amewaambia hasa nini cha kufanya kuhusu waimbaji"

alikuwa upande wa mfalme kwa habari zote za watu.

"upande wa mfalme wa Kiajemi kama mshauri katika mambo yote yanayohusu watu wa Kiyahudi"

Nehemiah 11:25

Kiriath-arba.....Diboni.....Yekabzeeli..... Yeshua.....Molada.......Beth-Peleti.....Hazar-Shuali....Beersheba

Hizi ni majina ya maeneo.

Nehemiah 11:28

waliishi

Hapa "wao" inahusu watu wa Yuda.

iklagi.....Mekona......9Enrimoni......Sora....Yarmuthi ....Zanoa....Adulamu.....Lakishi....Azeka.....Beer-sheba.....bonde la Hinomu

Hizi ni majina ya maeneo.

Nehemiah 12

Nehemiah 12:1

ambaye alikuja

"ambaye aliwasili kutoka Babeli"

pamoja na Zerubabeli

"chini ya uongozi wa Zerubabeli"

Zerubabeli....Shealueli....Yoshua....Seraya....Yeremia, Ezra.....Amaria.....Maluki....Hatushi.....Shekania, Harimu.....Meremothi

Haya ni majina ya wanaume.

Nehemiah 12:4

Sentensi Unganishi

Orodha ambayo ilianza katika 12 :1 inaendelea.

Kulikuwa

Maneno haya yameongezwa kwa tafsiri hii. Ikiwa utaendelea na orodha iliyoanza 12:1, unaweza kufuta maneno haya.

Iddo.....Ginethoni.....Abiya....Miyamini....Maazia.... Bilgai.....Shemaya....Yoyaribu.......Yedaya.....Salu...Amoki... Hilkia.....Yedaya

Haya ni majina ya wanaume.

Ginethoni

Ginethoni inaweza kuwa aina nyingine ya jina '"Ginethoni"

Nehemiah 12:8

Yeshua.....Binui.....Kadmieli.....Sherebia.....Yuda, .....Matania...Bakbukia.....Uno

Haya ni majina ya wanaume.

walisimama pembeni yao wakati wa huduma.

Inawezekana maana ni 1) hii ilikuwa wakati wa huduma ya ibada na hizi zilikuwa makundi mawili ya waimbaji (angalia UDB) au waabudu wengine, au 2) makundi haya walilinda hekalu kwa nyakati tofauti, au "kugeuka kuzingatia hekalu".

Nehemiah 12:10

Yoshua...Yoyakimu... Eliashibu...Yoyada...onathani...Yadua

Haya ni majina ya wanaume

Yoshua alikuwa babaye Yoyakimu

Ikiwa msomaji wako atahitaji kujua kwamba Jeshua alikuwa kuhani mkuu miaka mingi kabla ya wakati huu, unaweza kutaka kufuata mfano wa UDB. AT "Jeshua miaka mingi hapo awali alikuwa kuhani mkuu. Alikuwa baba ya Yoyakimu."

Nehemiah 12:12

Yoyakimu...Meraya.... Hanania....Meshulam...Yehohanani ....Yusufu

Haya ni majina ya wanaume.

Seraya.....Yeremia...Ezra....Amaria....Maluki... Shekania

Haya ni majina ya familia inayoitwa baada ya wanaume.

Nehemiah 12:15

Sentensi Unganishi

Orodha iliyoanza 12:12 inaendelea.

Adna...Helkai....Zekaria.....Meshulamu....Zikri ....Piltai....Shamua..... Yehonathani.....Matenai....Uzi.....Kalai.....Eberi .....Hashabia....Nethanel

Haya ni majina ya wanaume wote.

Harimu.....Meremothi...Ido....Ginethoni.....Abia.... Miyaamini....Maazia.....Bilgai....Shemaya....Yoyaribu.... Yedaya.....Salu.... Amoki...Hilkia.....Yedaya

Haya ni majina ya familia ambazo zinaitwa baada ya wanaume.

alikuwa kiongozi wa

"alikuwa kiongozi wa familia ya" au "alikuwa kiongozi wa wazao wa"

Meshulamu alikuwa kiongozi wa Ginethoni

Ginethoni inaweza kuwa aina nyingine ya jina la Ginethoi.

wa Miyaamini

Maandishi ya Kiebrania yanatoka kwa makosa jina la kiongozi wa familia ya Miniamin. Baadhi ya matoleo ya kisasa huacha maneno hayajahitimishwa, kama ULB inavyofanya. Matoleo mengine hutoa maelezo mafupi ya kufanya upungufu wa jina la kiongozi (tazama UDB).

Maazia

Maazia inaweza kuwa aina nyingine ya jina la Maazia

Nehemiah 12:22

Eliashibu....Yoyada......Yohana...... Yadua

majina ya wanaume

wakati wa utawala wa Dariyo

Maana nyingine inaweza kuwa ni "mpaka utawala wa Dariyo"

waliandikwa katika Kitabu cha tarehe

Hii inaweza kutaja Kitabu cha Mambo ya Nyakati. Waandishi waliandika maneno katika mistari hapo juu katika kitabu kilichoandika matukio ya kila siku.

hadi siku za Yohana mwana wa Eliashibu.

Kumbukumbu za hekalu zimeandikwa tu hadi Johana.

Nehemiah 12:24

kutii amri ya Daudi

Mfalme Daudi aliwaamuru Walawi jinsi walivyopaswa kuandaa na kuabudu ibada.

waliokuwa wamesimama mbele yao kumtukuza na kumshukuru, akijibu sehemu kwa sehemu

Hii inahusu jinsi walivyo imba baadhi ya nyimbo zao katika ibada. Kiongozi au kikundi kimoja angeimba maneno, kisha kikundi kimoja au viwili ambacho "vinasimama kinyume nao" ingeweza kuimba maneno katika jibu.

katika siku za Yoyakimu.....Yosadaki, na katika siku za Nehemiya, gavana na Ezra.....mwandishi

Tarehe hiyo ilikuwa imefungwa kwa kutaja wale ambao walikuwa wakiongozwa na Wayahudi wakati huo. 'wakati Yehoyakimu ... Yehozadaki alikuwa kuhani mkuu, na wakati Nehemia alikuwa gavana na Ezra ... alikuwa mwandishi'

Hashabia, Sherebia..... Yeshua....Kadmieli....Daudi....Matania, Bakbukia, Obadiya, Meshulamu, Talmoni na Akubu....Yoyakimu....Yoshua....Nehemia....Ezra

Haya ni majina ya wanaume.

Nehemiah 12:27

Katika kujitolea kwa ukuta wa Yerusalemu

Maana iwezekanayo ni 1) "Wakati walipojitolea ukuta wa Yerusalemu" au 2) "Kwa hiyo ukumbi wa Yerusalemu ukatekelezwa."

ngoma

mbili nyembamba, sahani ya chuma ya pande zote ambazo huunganishwa pamoja ili kutoa sauti kubwa

Nehemiah 12:29

Beth-gilgali.....Geba na Azmawethi

Haya ni majina ya maeneo.

Nehemiah 12:31

viongozi Yuda

viongozi wa watu waliokuwa wakiishi katika mkoa wa Yuda

Nehemiah 12:32

Hoshaya....Azaria....Ezra....Meshulamu....Yuda.... Benyamini... Shemaya....Yeremia....Zekaria....Yonathani.... Shemaya....Mataniya.....Mikaya.....Zakur....Asafu

Haya ni majina ya wanaume.

na baada yake akaenda

"na nyuma yao walimfuata"

na wana wa makuhani waliokuwa na tarumbeta, na Zekaria

Matoleo mengine yanasoma, "na kati ya makuhani na tarumbeta, Zekaria"

Zekaria mwana wa Yonathani mwana wa Shemaya mwana wa Mataniya mwana wa Mikaya mwana wa Zakuri mwana wa Asafu.

Majina yote baada ya "Zekaria" ni mababu wa Zakaria. Orodha hii inaunganisha Zakaria na mwimbaji maarufu Asafu. "Zekaria, mwana wa Yonathani, mwana wa Shemaya, mwana wa Matania, mwana wa Mikaya, mwana wa Zakuri, mwana wa Asafu."

Nehemiah 12:36

Pia kulikuwa

"Pamoja nao walikuwa"

Zekaria.....Shemaya, Azareli, Milalai, Gilalai, Maai, Nethaneli, Yuda, Hanani....Daudi.... Ezra

Haya ni majina ya wanaume.

Ezra mwandishi alikuwa mbele yao

"Ezra mwandishi alikuwa akiwaongoza"

Lango la Chemchemi...... Lango la maji

Haya ni majina ya wazi katika ukuta.

Nehemiah 12:38

kwaya

"kundi la waimbaji"

Niliwafuata

Nehemia aliwafuata

mnara wa vinyago...mnara wa Hananeli... mnara wa Hamea

Hizi ni majina ya miundo mirefu ambako watu walikuwa macho kulinda hatari .

Ukuta mrefu

Hili ni jina la sehemu ya ukuta.

lango la Efraimu...lango wa kale....lango la samaki... lango la Kondoo...lango la walinzi

Haya ni majina ya wazi katika ukuta.

Nehemiah 12:40

mimi pia nikachukua nafasi yangu

Nehemia anasema hapa. AT "Mimi, Nehemia, pia nilichukua nafasi yangu"

Eliakimu.... Maaseya.....Miyamini.....Mikaya....Elioenai.... Zekaria....Hanania ....Maaseya....Shemaya...Eleazari....Uzi....Yehohanani ....Malkiya, Elamu.....Ezeri

Haya ni majina ya wanaume ambao walikuwa makuhani wakati huo.

Yezrahia

Hili ni jina la kiume ambaye alikuwa kiongozi wa waimbaji.

walijifanya wenyewe kusikia

"kuimba kwa sauti kubwa"

Nehemiah 12:43

shangwe na furaha kubwa

"shangwe sana"

Hivyo furaha ya Yerusalemu ikasikiwa toka mbali

"Yerusalemu" ni mfano wa "sauti ambayo watu wa Yerusalemu walifanya." Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu ya kazi. AT "watu mbali mbali na Yerusalemu waliweza kusikia sauti ambayo watu wa Yerusalemu walifanya wakati wa kusherehekea"

Nehemiah 12:44

wanaume waliteuliwa kuwa wasimamizi

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. Haijulikani ambaye aliwachagua wanaume. AT "walichagua wanaume kuwa wajibu"

michango

mambo watu waliwapa makuhani

Kwa maana Yuda walifurahi juu ya makuhani na Walawi

Inaonekana kwamba watu waliwachagua wanaume kwa sababu watu wa Yuda waliwashukuru kwa makuhani na Walawi ambao walikuwa wakihudumia.

waliokuwa wamesimama mbele yao

Walawi na makuhani hawakuwa wamesimama tu, walikuwa wakifanya kazi zao. Maana yanaweza kufanywa wazi. AT "ambao walikuwa wamesimama mbele yao wakimtumikia Mungu."

Walinzi wa malango

watu waliopewa kila mlango, wajibu wa kudhibiti shughuri zote za jiji au hekalu, na kufungua na kufunga milango kwa nyakati na kwa sababu zilizowekwa na msimamizi. Tafsiri kama katika 7:1.

Nehemiah 12:46

kulikuwa na wasimamizi wa waimbaji

Sentensi hii inaeleza kwa nini watu walifanya kile walichofanya katika 12:44 na kutupa habari zaidi juu ya wakati ambapo Daudi aliwaambia watu jinsi ya kuabudu hekaluni.

Katika siku za Zerubabeli

Zerubabeli alikuwa mzao wa Mfalme Daudi na mmoja wa watawala katika eneo la Yuda.

Wakaweka pembeni sehemu

"Israeli wote wakaweka pembeni sehemu"

walinzi wa malango

watu waliopewa kila mlango, wajibu wa kudhibiti shughuri zote za jiji au hekalu, na kufungua na kufunga milango kwa nyakati na kwa sababu zilizowekwa na msimamizi. Tafsiri kama katika 7:1.

wana wa Haruni

makuhani katika Israeli, ambao walitoka kwa Haruni, ndugu wa Musa

Nehemiah 13

Nehemiah 13:1

katika masikio ya watu

"ili watu waweze kuisikia"

anapaswa kuja katika kusanyiko la Mungu, milele

"lazima aingie katika kanisa la Mungu"

Hii ilikuwa kwa sababu

"Hawakuweza kuingia kanisani kwa sababu"

Nehemiah 13:4

Eliashibu kuhani akawekwa

Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu ya kazi. AT "walimchagua Eliashibu kuhani" au "viongozi wamteua Eliashibu kuhani"

Alikuwa na uhusiano na Tobia

"Eliashibu na Tobia walifanya kazi pamoja"

Eliashibu alimuandalia Tobia chumba kikubwa

"Eliashibu aliandaa chumba kikuu cha duka kwa Tobia kutumia"

Walinzi wa malango

watu waliopewa kila mlango, wajibu wa kudhibiti shughuri zote za jiji au hekalu, na kufungua na kufunga milango kwa nyakati na kwa sababu zilizowekwa na msimamizi. Tafsiri kama katika 7:1.

Nehemiah 13:6

Lakini wakati huu wote sikuwepo Yerusalemu

"Wakati huo yote haya yalitokea, nilikuwa mbali na Yerusalemu"

mabaya ambayo Eliashibu alikuwa amefanya kwa kumpa Tobia chumba cha kuhifadhi katika mahakama ya nyumba ya Mungu

Hiki ilikuwa chumba ambacho hapo awali kilikuwa kitakasolewa kuhifadhi vitu vya sadaka (13:4).

Nehemiah 13:8

Hasira

"Kukasirika" au "kupata hasira" ina maana ya kutofurahishwa au kuhangaishwa juu ya jambo fulani au mtu fulani. - Watu wanapokasirika ni dhambi na ubinafsi lakini wakati mwingine kuna hasira ya haki dhidi ya udhalimu au mateso. - Hasira ya Mungu inaelezea namna ambavyo hapendezwi na dhambi. - "kuwatia hasira" maana yake ni "kuwasababisha wakasirike"

nyumba

Neno "kaya" linamaanisha watu wote wanaoishi pamoja katika nyumba, ikiwa ni pamoja na wajumbe wa familia na watumishi wowote wanao. .Ikiwa mtu anaweza kusimamia nyumba, hii itahusisha kuongoza watumishi pamoja na kutunza mali. Wakati mwingine "familia" inaweza kutaja mfano wa familia nzima ya mtu, hasa wazao wake.

safi, kusafisha, kusafisha

Kuwa "safi" inamaanisha kuwa na udhaifu au kuwa na chochote kilichochanganywa katika hiyo haipaswi kuwepo. Kutakasa kitu ni kusafisha na kuondoa kitu chochote ambacho kinaathiri au kinaipotosha. Kuhusu sheria za Agano la Kale, "kusafisha" na "kusafisha" hutaja hasa kutakasa kutoka kwa mambo ambayo hufanya kitu au mtu asiye najisi, kama vile ugonjwa, maji ya mwili, au kuzaliwa. Agano la Kale pia lilikuwa na sheria kuwaambia watu jinsi ya kutakaswa kutoka kwa dhambi, kwa kawaida kwa dhabihu ya mnyama. Hii ilikuwa ya muda mfupi na dhabihu ilibidi kurudia tena na tena. Katika Agano Jipya, kutakaswa mara kwa mara ina maana ya kutakaswa kutoka kwa dhambi. Njia pekee ambayo watu wanaweza kuwa safi na kudumu kutoka kwa dhambi ni kupitia kutubu na kupokea msamaha wa Mungu, kwa kuamini Yesu na dhabihu yake.

Nyumba ya Mungu, Nyumba ya Bwana

Katika Biblia, maneno "nyumba ya Mungu" (nyumba ya Mungu) na "nyumba ya Yahweh (nyumba ya Bwana) inaelezea mahali ambapo Mungu anaabudu Neno hili pia linatumiwa hasa kwa kutazama hema au hekaluni. Wakati mwingine "nyumba ya Mungu" hutumiwa kutaja watu wa Mungu.

sadaka ya nafaka

Sadaka ya nafaka ilikuwa zawadi ya unga wa ngano au shayiri iliyotolewa kwa Mungu, mara nyingi baada ya sadaka ya kuteketezwa. Mbegu iliyotumiwa kwa ajili ya sadaka ya nafaka ilitakiwa kuwa nzuri. Wakati mwingine ilikuwa kupikwa kabla ya kutolewa, lakini mara nyingine iliachwa bila kupikwa. Mafuta na chumvi ziliongezwa kwenye unga wa nafaka, lakini hakuna chachu au asali iliruhusiwa. Sehemu ya sadaka ya nafaka iliteketezwa na sehemu yake ilikuwa kuliwa na makuhani.

uvumba

Neno "uvumba" linamaanisha mchanganyiko wa manukato yenye harufu nzuri ambayo huteketezwa kuzalisha moshi ambayo ina harufu nzuri. Mungu aliwaambia Waisraeli kufukiza uvumba kama sadaka kwake. Ya uvumba ilipaswa kufanywa kwa kuchanganya kiasi sawa cha viungo vitano maalum kama vile Mungu alivyoagiza. Hii ilikuwa uvumba mtakatifu, kwa hivyo hawakuruhusiwa kuitumia kwa sababu nyingine yoyote. "Madhabahu ya uvumba" ilikuwa madhabahu maalum ambayo ilikuwa tu kutumika kwa kuchoma uvumba Mafuta hayo yalitolewa angalau mara nne kwa siku, kila saa ya sala. Pia ilitolewa kila wakati sadaka ya kuteketezwa ilitolewa. Kuungua kwa uvumba kunawakilisha sala na ibada inayoinuka kwa Mungu kutoka kwa watu wake Njia nyingine za kutafsiri "uvumba" zinaweza kujumuisha, "manukato yenye harufu nzuri" au "mimea nzuri ya kupendeza."

Nehemiah 13:10

sehemu zilizotolewa kwa ajili ya kuwapa Walawi hazikutolewa kwao

Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu ya kazi. AT "watu hawajawaingiza ndani ya vituo vya kuhifadhi sehemu yao ya kumi na sadaka ya chakula kwa makuhani wa hekalu"

walikuwa wamekimbia, kila mmoja katika shamba lake, Walawi na waimbaji waliofanya kazi hiyo

"Walawi na waimbaji waliofanya kazi waliondoka hekalu, kila mmoja kwenda shamba lake mwenyewe"

Kwa nini nyumba ya Mungu imeachwa?

Hili ndio swali la kuzingatia tangu Nehemia analitumia ili kuwapinga au hata kuwadhihaki viongozi ambao hawakuwa wamefanya kazi yao

Nehemiah 13:12

Yuda wote

Jina la ardhi ni metonim kwa watu wa nchi. Huenda hii ni kizazi. AT "watu wote waliokaa Yuda"

Shelemia....Sadoki...Pedaya... Hanani...Zakuri...Matania

Haya ni majina ya wanaume

walihesabiwa kuwa waaminifu

Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu ya kazi. Maana nyingine ya "mwaminifu" linaweza kutafsiriwa kama kitenzi. AT "nilijua kwamba ningeweza kuwaamini"

Nikumbuke, Ee Mungu wangu, juu ya hili

"Mungu wangu, unikumbuke juu ya hili."

Nehemiah 13:15

waliokanyaga mvinyo

Neno "vikwazo vya divai" ni mshikamano wa zabibu ambazo zilikuwa kwenye vipaji vya mvinyo. Watu walikuwa wakitembea kwenye zabibu ili kupata juisi kutoka kwao ili kufanya divai. AT "akitembea juu ya zabibu katika vikombe vya divai"

kunyaga

kutembea kwenye kitu cha kuponda au kushinikiza

Nehemiah 13:16

Tiro

jina la mji

Je! ni ubaya gani huu mnafanya, kuinajisi siku ya Sabato

Nehemia ni kuwapiga viongozi wa Yuda. Hii inaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Unafanya jambo baya kwa kudharau siku ya Sabato." au "Mungu atawaadhibu kwa kufanya jambo hili baya, kwa kudharau siku ya Sabato."

Je! Baba zenu hawakufanya hivyo?

Nehemia anawatia viongozi wa Yuda. Hii inaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Unajua kwamba baba zako walifanya hivyo, na ndiyo sababu Mungu alileta uovu huu wote juu yetu na juu ya mji huu."

Nehemiah 13:19

Mara ilipokuwa giza..... kabla ya Sabato

"Wakati jua lilishuka ... na ilikuwa ni wakati wa Sabato kuanza"

milango ifungwe na kwamba haifai kufunguliwa hadi

Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu ya kazi. AT "kwamba walinzi wafunga milango na hawafunguli mpaka "

mzigo wowote usiweze kuletwa

Hii inaweza kutafsiriwa kwa fomu ya kazi. AT 'hakuna mtu anayeweza kuleta vitu walivyotaka kuuza'

wauzaji wa kila aina ya bidhaa

"watu ambao walileta vitu vingi ambavyo walitaka kuuza"

Nehemiah 13:21

Mbona mnakaa nje ya ukuta?

Nehemia anafanya swali hili lisipate jibu bali kuwaadhibu wafanyabiashara na kusisitiza amri yake. AT "Wewe ni kambi nje ya ukuta dhidi ya kile nilichoamuru."

nitakuweka mikononi!

Neno "mikono" ni metonymy kwa hatua kali. AT 'Nitawafukuza kwa nguvu!" au "Nitawaondoa kwa nguvu!"

Nehemiah 13:23

Sentensi Unganishi

Aya hizi zinaonyesha hatua inayofuata.

Wayahudi waliokuwa wameoa wanawake wa Ashdodi, Amoni na Moabu

"Wayahudi ambao walikuwa wameoa wanawake wa kigeni" Mungu alikuwa amekataa kuoa ndoa.

Ashdodi

Jina la mji

Amoni...Moabu

majina ya mataifa

Nusu ya watoto wao

"Matokeo yake, nusu ya watoto wao"

Nehemiah 13:25

Nami nikawasiliana nao

"Nilizungumza moja kwa moja nao juu ya kile walichofanya"

nikawapiga baadhi yao

kwa mikono yake

Naliwaapisha kwa Mungu

"Nimewafanya wanasema ahadi mbele ya Mungu"

Je, Sulemani mfalme wa Israeli hakufanya dhambi kwa sababu ya wanawake hawa?

Nehemia anawaangamiza wanaume. Hii inaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Unajua kwamba Sulemani mfalme wa Israeli alifanya dhambi kwa sababu ya wanawake hawa."

Je, tunapaswa kukusikiliza na kufanya uovu huu hata kumhalifu Mungu wetu na kuwaoa wanawake wageni?

Nehemia anawaangamiza wanaume. Hii inaweza kutafsiriwa kama taarifa. AT "Hatutawasikiliza au kufanya uovu huu mkubwa au kutenda kwa uongo dhidi ya Mungu wetu kwa kuoa wanawake wa kigeni."

Nehemiah 13:28

Yoyada....Eliashibu...Sanbalati

Haya ni majina ya wanaume

Mhoroni

mtu kutoka mji wa Beth...Horoni

nilimondoa kutoka mbele yangu

"Nilimfukuza" au "nimemfanya aondoke Yerusalemu"

Wakukumbushe

"Fikiria juu yao" au "Kumbuka kile walichofanya"

wameunajisi ukuhani

"wamekufanya ufikirie juu ya makuhani na kazi yao kama kwamba walikuwa wachafu"

na agano la ukuhani na Walawi

"wamekufanya ufikirie juu ya agano ulilofanya na makuhani na Walawi kama kwamba ni safi"

Nehemiah 13:30

Kwa hiyo nimewatakasa

"Kwa njia hii niliwatakasa"

kuimarisha kazi za makuhani na Walawi

"aliwaambia makuhani na Walawi nini walipaswa kufanya"

Nilitoa sadaka za kuni

"Nilipangwa kwa ajili ya utoaji wa kuni kwa ajili ya sadaka za kuni"

matunda ya kwanza

"kwa sadaka ya matunda ya kwanza wakati wa mavuno"

Nikumbuke, Mungu wangu, kwa mema

"Fikiria juu ya yote niliyoyatenda, Mungu wangu, na kunibariki kwa sababu ya mambo mema ambayo nimeyafanya"

Esther 1

Esther 1:1

Katika siku za Ahasuero

"Katika wakati wa Ahasuero" au "wakati Ahasuero alipokuwa akitawala kama mfalme."

127

(Tazama: tafsiri nambari)

majimbo

"Jimbo" ni sehemu kubwa ambayo katika hiyo baadhi ya nchi zimegawanywa kwa makusudi ya serikali.

Ngome

Ngome, boma au kambi iliyoimarishwa.

Shushani

Mji wa utawala wa wafalme wa Uajemi.

Esther 1:3

mwaka wa tatu

"baada ya miaka 2"

180

(Tazama: tafsiri nambari)

Esther 1:5

Saba

"7"

ikulu

tumia neno lile lililotumika katika 1:1.

Shushani

Tumia neno lile lilelililotumika katika 1:1.

Esther 1:7

ukarimu

"utayari mkubwa wa kuwapa"

Mfalme alikuwa amewaamuru wahudumu wake wote wa ikulu kuwatenda vyovyote kila mgeni alivyotaka

kauli hii inamaanisha kwamba mfalme aliwaambia wafanyakazi wake kuwapa wageni wote ambao walio wataka.

Esther 1:9

siku ya saba

"baada ya siku 6"

wakati moyo wa mfalme ulipokuwa ukijisikia fu kwa sababu ya mvinyo

"baada ya mfalme alipokuwa amelewa kwa mvinyo"

Mahumani, Biztha, Harbona, Bigtha, Abagatha, Zethari na Karkas

(Tazama: Tafsiri majina)

saba

"7"

Esther 1:12

Kwa nini mfalme alikasirika sana?

Mfalme alikasirika sana kwa sababu Malkia Vashiti alikataa kuja kama mfalme alivyokuwa ameagiza.

Esther 1:13

Carshena, Shethar, Admatha, Tarshish, Meres, Marsena na Memucan

(Tazama: tafsiri majina)

saba

"7"

katika kutekeleza sheria

"Katika kutekeleza sheria au katika kutii sheria

Esther 1:16

Mumekani

(Tazama: tafsiri majina)

Majimbo

Tumia neno lile lile lililotumika katika 1:1.

Esther 1:19

wote/kubwa mno

"kubwa" au "kubwa sana"

Esther 1:21

Memkani

(Tazama: tafsiri majina)

jimbo

Tumia neno lile lile lililotumika katika 1:1.

Esther 2

Esther 2:1

tangazo/ mbiu

Hii inarejea kwenye tangazo katika 1:19.

Esther 2:3

Majimbo

Tumia neno lile lile lililotumika katika 1:1.

haremu

"mahali ambapo wake wa watawala wanatunzwa"

ikulu

Tumia neno lile lile lililotumika katika 1:5.

Sushani

Tumia neno lile lile lililotumika katika 1:1.

Hegai

(Tazama: tafsiri majina)

vipodozi vyao

"Kipodozi" in kitu kama kirimu, losheni, au poda ambayo mara nyingi wanawake ujipaka katika uso au mwili ili kupendezesha muonekano wao.

Esther 2:5

Sushani

Tumia jina lile lile lililotumika katika 1:1.

mwana wa Jaira mwana wa Shimei mwana wa Kishi

'"Jaira," "Shimei" na"Kishi" ni wanaume ambao "Modekai" ni mwana wa kiume anatoka.

Mbenjamini

"wa kabila la Benjamini"

Alikuwa amechukuliwa kutoka Yerusalemu

Andiko la Kiebrania haliweki wazi anayezungumziwa hapa. Pengini ni Kishi, ambaye inaonekana alikuwa baba yake na babu wa Modekai. Kama ilikuwa Modekai mwenyewe, hivyo angekuwa mzee sana kwa wakati wa matukio yanayomhusu Esta. Matoleo mengi ya kisasa haziliweki wazi hili. Ni matoleo machache likiwemo la UDB, linahisi kuwa Modekai ndiye aliyekuwa amechukuliwa kutoka Yerusalem.

Yekonia, mfalme wa Yuda

(Tazama: tafsiri majina)

Esther 2:7

Hadasa

Hili ni jina la Kiebrania la Esta.

binti wa mjomba wake

"binamu yake'

Hakuwa na baba wala mama

"baba na mama yake walikufa"

Esther 2:8

alitangaza

"alitangaza"

ikulu

Tumia neno lile lile lililotumika katika 1:5.

Esther 2:10

kuhusu habari ya Esta

"vile ambavyo Esta alivyokuwa akiendelea" au "kuhusu hali ya Esta"

Esther 2:12

kufuata maelekezo kwa ajili ya wanawake

"kutenda sawa sawa na ni mahitaji kwa ajili ya wanawake"

ya matibabu ya urembo

Mambo yafanywayo ili kuwafanya wasichana kuonekana warembo zaidi na kunukia vizuri.

vipodozi

Tumia neno lile lile lililotumika katika 2:3.

ikulu

Tumia neno lililotumia katika 1:5.

Esther 2:14

wakati wa ahsubuhi

"ahsubuhi inayofuata"

nyumba ya pili

"nyumba nyingine"

msimamizi

"kuangalia" au "ulinzi"

Shaashigazi

(Tazama: tafsiri majina

Esther 2:15

Abihali

"Abihaili"alikuwa baba yake na Esta na mjomba wa Modekai.

Hegai

Tumia neno lile lile liliotumika katika 2:3

mwezi wa kumi, ambao ni mwezi wa Teneti

"Tibeti" ni jina la mwezi wa kumi kwa kalenda ya Kiebrania. Ni wakati wa sehemu ya mwisho wa Desemba na sehemu ya kwanza ya January kwa kalenda ya Magharibi.

mwaka wa saba

"mwaka namba7"

Esther 2:17

mfalme alipenda

Hili ni neno la kihisia la "upendo".

ushuru

"ukusanyaji wa ushuru"

majimbo

Tumia neno lile lile lililotumika katika 1:1

Esther 2:19

mara ya pili

"mara moja zaidi" au"muda mwingine"

alimuelekeza

"alimwambia"

Bigthani na Tereshi

Haya yalikuwa majina ya walinzi wawili waliolinda ikulu.

Esther 2:22

mti

umbo ambalo mtu hunyongwa kwa kufunga kamba shingoni mwake na kuuning'niza mwili pasipo msaada wowote chini.

Esther 3

Esther 3:1

Hamani mwana wa Hammedatha Mwagagi

Hili ni jina na wadhifu wa Hamani, mmoja wa wasimamizi wa mfalme.

aliweka kiti chake cha mamlaka

"alipandisha cheo"

walijinyenyekezea kwa Hamani

"Walijinyenyekeza na kulala kifudifudi juu ya ardhi mbele ya Hamani"

Esther 3:3

amrisha, kuamrisha, amri

Neno "kuamrisha" maana yake kumuagiza mtu kufanya kitu. "Amuru" au "amri" ni kile ambacho mtu aliagizwa kufanya.

Myahudi, Uyahudi, Wayahudi

Wayahudi ni watuambao ni uzao wa mjukuu wa Abrahamu, Yakobo. Neno "Myahudi" linatokana na neno "Yuda."

Esther 3:5

Hakupenda kwa wazo la kumuua Modekai pekee

"Alikataa wazo la kumuua Modekai pekee"

Kuwakatilia mbali Wayahudi

"kuwaondoa Wayahudi wote" au "Kuwakatilia mbali Wayahudi wote"

Esther 3:7

Katika mwaka wa kwanza (ambao ni mwezi wa Nisani)

"Nisani" ni jian la mwezi wa kwanza wa kalenda ya Kiebrania. Ni sehemu ya mwisho ya wakati wa Machi na sehemu ya kwanza ya Aprili kwa kalenda ya Kimagharibi.

wakapiga Puri/ kura

"wakapiga kura"

mwezi wa kumi na mbili (mwezi wa Adari)

"Adari" ni jina kumi na mbili na mwezi wa mwisho wa kalenda ya kalenda ya Kiebrania. Ni wakati wa mwisho wa sehemu ya mwisho ya Februari na sehemu ya kwanza ya machi katika kalenda za Magharibi.

Esther 3:8

watu fulani

"kikundi cha watu"

majimbo

Tumia neno lile lile lililotumikka kama lilivyotumika katika 1:1

talantaelfu kumi za fedha

"talanta 10,0000 za fedha"

Esther 3:10

pete ya muhuri

pete maalum ambaye ilitumiwa kugonga nyalaka za Mfalme kwenye matangazo.

Esther 3:12

siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kwanza

Huu ni mwezi wa kwanza wa Kalendda uya Kebrania. Siku ya kumi na tatu ni karibu na mwanzo wa Mwezi Aprili katika kalenda za Magharibi.

wasimamizi wa majimbo wa mfalme

"wasimamizi wa majimbo" Tumia neno lile lile lililotumika kwa jimbo katika 1:1.

siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kumi na mbili (ambao ni mwezi wa Adari)

Adari" ni jina la kumi na mbili na mwezi wa mwisho wa kalenda ya Kiebrania. Kumi na tatu ni karinu na mwanzo wa machi kwa kalenda za Magharibi.

Esther 3:14

jimbo

Tumia neno lile lile katika 1:1

Shushani

(Tazama: tafsiri majina)

ulikuwa katika msukosuko

"ulikuwa katika hai ya msukosuko mkubwa"

Esther 4

Esther 4:1

jimbo

Tumia neno lile lile kama lililotumika katika 1:1.

Esther 4:4

majonzi

"mahangaiko makubwa"

Hathaki

(Tazama: tafsiri majina)

Esther 4:6

Hathaki

(Tazama: tafsiri majina)

mbele ya lango la mji

" soko"

Hamani

Tumia neno lilelile kama liliotumika katika 3:1.

Esther 4:9

siku thelathini

"siku 30"

Esther 4:13

Ni nani ajuaye kama umekuja katika nafasi hii kwa wakati muafaka kama huu?

Kusudi la swali hili ni kumfanya Esta kufikiri kwa undani kuhusu nafasi yake katika swala hili. "Ni nani ajuaye, pengineiikuwa kwa muda kama huu kwamba ulifanywa kuwa malkia."

Esther 4:15

Shushani

Tafsiri kama katika 1:1.

siku tatu

"siku 3"

Esther 5

Esther 5:1

siku tatu

"siku 3"

Esther 5:3

Hamani

Tafsiri kama katika 3:1

kwa ajili yake

"kwa ajili ya mfalme"

Esther 5:5

hitaji

"ombi kwa mfalme"

utapewa

"ombi lako utapewa"

Esther 5:7

ikikupendeza, inayopendeza, upendeleo

Neno ikikupendeza" inamaanisha kufanya kitu kunufaisha mtu ambaye ameheshimiwa.

kuheshimu

Neno heshimu" inamaanisha kumpa mtu heshima.

Esther 5:9

hasira

"hasira kali"

Zereshi

(Tazama: tafsiri majina)

Esther 5:12

haya yote sio kitu kwangu

"halinifanya mimi kufurahia" au " hainitoshelezi"

Esther 5:14

miti

tafsiri kama katika 2:22

futi hamsini

"futi 50"

Esther 6

Esther 6:1

Bigithatna na Tereshi

Tafsiri kama katika 2:19

"walinzi wawili wa mfalme"

"wasimamizi 2 wa mfalme"

Hakufanyiwa kitu chochote

Mfalme hakufanya chochote kwa Modekai."

Esther 6:4

Hamani

Tafsiri kama katika 3:1

ua wa nje

"ua wa kwanza kutoka nje"

kumtundika Modekai

"kumweka Modekai kwenye kifo kwa kumtundika"

miti ya kutundikia

Tafsiri hili kama katika 2:22

kuweka

"kujenga"

akasema moyoni mwake

"akafikiri mwenyewe"

Ni nani ambaye mfalme apenda kumuheshimu zaidi yangu?

'Hakika hakuna mwingine ambaye mfalme apenda kumuheshimu zaidi yangu!"

Esther 6:7

mavazi ya kifalme yaletwe

"watumishi walete mavazi ya kifalme"

ametumiwa/ameendeshwa

"Hii ni sentensi ya wakati uliopita wa endesha"

taji ya kifalme

umbo maalum iliyowakilisha familia ya mfalme

Hivyo mavazi na farasi apewe

"Hivyo mpe mavazi na farasi"

Watangaze

"Watumishi na wasimamizi wakuu watangaze"

Esther 6:10

Modekai

Modekai alikuwa mwanamme myahudi akiishi katika nchi ya Waajemi. Alikuwa mlezi wa binamu yake Esta, ambaye baadaye alikuwa mke wa mfalme wa Uajemi, Ahausiero.

Muyahudi, Wayahudi

Wayahudi ni uzao wa mjukuu wa Abrahamu, Yakobo. Neno Yahudi linatokana na neno Yuda.

lango, komeo

"lango" ni kizuizi kilichowekwa mahali pa kuingilia katika fensi au ukuta unaozunguka nyumba.Komeo inamaanisha ubao au chuma ambacho kinaweza kusogezwa katika sehemu ili kufunga lango.

tangaza, mbiu

ni kutangaza au kutangaza kitu kwenye hadhara na kwa ujasiri.

Esther 6:12

Zereshi

(Tazama: tafsiri majina)

Esther 7

Esther 7:1

Hamani

Tafsiri kama katika 3:1

katika siku ya pili

"katika karamu hii ya 2"

haja/ombi

tafsiri kama katika 5:5

utapewa

"nitakupa"

Esther 7:3

machoni pako

"kutoka kwako"

nipewe

"nihudumiwe"

Kwa kuwa tumeuzwa

"Kwa kuwa mbiu imetuuza sisi"

tuharibiwe, tuuwawe na tuangamizwe

Maneno haya matatu yana maana moja ila yametuika kuweka msisitizo.

Esther 7:6

Hofu

"woga mkubwa"

hasira

"hasira kali"

Esther 7:8

mvinyo ulikuwa umetengwa

"watumishi walikuwa wameleta mvinyo"

kochi

kipande kirefu cha samani ambapo mtu hukaa au kulala.

atamdharirisha malkia

Hii neno ni namna ya upole ya kuuliza kama atashika na kulala naye.

Atamdharirisha malkia mbele yangu katika nyumba yangu?

"Unajaribu kumdharirisha malkia wakati akiwa hapa nami katika ikulu yangu!"

watumishi wakamfunga Hamani uso

baadhi ya watumishi walifunga kichwa cha Hamani, kama walivyofanya watu walikuwa tayari kwa kutundikwa.

Esther 7:9

Haribona

Hili ni jina la mwanamme. (Tazama: tafsiri majina)

miti

Tazama jinsi ulivyotafsiri hili katika 2:22

futi hamsini

"futi 50"

Esther 8

Esther 8:1

Hamani

Tafsirfi kama katika 3:1

pete ya muhuri

pete maalum ambayo iliweza kutumiwa kupiga muhuri mbiu/ tangazo la Mfalme.

Esther 8:3

akasihi

"akaomba"

Mwagagi

Tafsiri kama katika 3:1

mpango ambao alikuwa ameupanga

"mbinu ambao alikuwa ameipangaa"

Esther 8:5

batilisha

"kufuta rasmi"

Hammedatha

(Tazama:tafsiri majina)

majimbo

Tafsiri kama katika 1:1.

Ninawezaje kuona ubaya ukiwapata watu wangu? Ninawezaje kutazama uharibifu wa jamaa zangu?

"Siwezikuvumilia kuona ubaya unawaangukia Wayahudi. Siwezi kuvumilia kutazama jamaa zangu wakiuwawa."

Esther 8:7

miti ilitumika kutindikia waharifu

Tafsirikama katika 2:22

Andika mbiu nyingine

Inamaanisha kuwa Moderkai na Esta waliandika barua.

haiwezi kutanguliwa

"hakuna mtu anaweza kuibatilisha" au" hakuna mtu awezaye kuifuta rasmi"

Esther 8:9

aliita

"alikusanya"

mwezi wa tatu, ambao ni mwezi wa Sivani, katika siku ya ishirini na tatu ya mwezi

siku ya tatu ya mwezi "sivani"ni jina la mwezi wa tatu katika kalenda ya Kiebrania, siku ya ishirini na tatuni kati katika ya mweziJuni kwa kalenda za Magharibi.

majimbo

Tazama jinsi ulivyotafisiri hii katika 1:1

127

(Tazama: tafsiri majina)

Esther 8:10

pete ya muuri

Tafsiri kama katika 3:1

matarishi

"watu wanaobeba ujumbe"

waliozaliwa kwa mfalme

ni farasi aliyestafishwa katika mashindano ambaye ametunzwa kwa ajili ya uzalishaji wa farasi wengine wa mashindano

ruhusa

"haki"

kukusanyika na kujilinda

Hili ni neno lililotumika likimaanisha kupigana wala sio kukimbia.

siku ya ishirini ya mwezi wa kumi na mbili, ambao ni mwezi wa Adari

Tazama jinsi ulivyotafsiri hii katika 3:12

Esther 8:13

kulipa kisasi

tendo la kumuumiza mtu aliyekuumiza.

Shushani

Tafsiri kama katika 1:1

Esther 8:15

nuru

"furaha"

jimbo

Tafsiri kama katika1:1

sikukuu

"maadhimisho"

Esther 9

Esther 9:1

mwezi wa kumi na mbili, siku ya kumi na tatu ambayo ni siku ya Adari katika siku ya kumi na tatu

Tazama jinsi ulivyotafsiri hili katika 3:12.

walitarajia kutekeleza

"tekeleza"

majimbo

Tafsiri kama katika 1:1.

kutia mikono juu ya wale waliokusudia ubaya juu yao

"kuwapiga maadui zao"

Esther 9:3

majimbo

Tafsiri kama katika 1:1.

maakida na magavana

"magavana wa majimbo"

umaarufu

"ukuu" au "kutambuliwa"

Esther 9:6

Shushani

Tafsiri kama katika 1:1.

ngome

ngome

wanaumemia tano

wanaume500.

Parishandatha, Dalphoni, Aspatha, Poratha, Adalia, Aridatha, Parimashita, Arisai, Aridai, Vaizatha

(Tazama: tafsiri majina)

wana kumi

"wana 10"

Hamani

(Tazama: tafsiri majina)

Hammedatha

(Tazama: tafsiri majina)

Esther 9:11

mji wa ngome

ngome

wanaume mia tano

wanaume 500

wana kumi

"wana 10"

Je wamefanya nini katika majimbo mengine?

"Ni nini walipaswa kufanya katika majimbo mengine ya mfalme!"

matakwa

"ombi"

Esther 9:13

wana kumi

"wana 10"

mti uilotumika ktundikia waharifu

tafsiri kama katika 2:22

Esther 9:15

siku ya kumi na nne ya mwezi wa Adari

Adari ni jina la mwezi wa kumi na mbili na mwezi wa mwisho kwa kalenda ya Kiebrania. Siku ya kumi na nne karibia na mwezi Machi.

Majimbo

Tafsiri hii kama ulivyotafsiri hii katika 1:1

elfu sabini na tano

sabini na tano 75000

Esther 9:17

siku ya kumi na tana ya mwezi wa Adari

Tazama ulitafsiri hii katika 3:12.

siku ya kumi na nne

Tazama vile ulivyotafsiri hii katika 915.

Shuani

Tazama ulivyotafsiri hii katika 1:1.

siku ya kumi na tano

"siku 15"

furaha

'shangwe"

Esther 9:20

siku ya kumi na nne na kumi na tano

"siku 14 na 15"

sikukuu

"maadhimisho" au "karamu"

Esther 9:23

Maelezo ya Jumla:

Aya hiiinafupisha sehemu kubwa ya simulizi ya Esta ii kufafanua sababu ya sherehe ya Purimu.

Hamani

(Tazama: tafsiri majina)

Hammedatha

(Tazama: tafsiri ya majina)

Mwagagi

Hawa ni watu wa kundi la Hamani.

alipiga Puri (alipiga kura)

"alipiga kura kubashiri ili kupata siku ya bahati katika mwaka ambayo atakayotekeleza mpango wake"

Puri

"Purimu au kura"

Lakini taarifa ilipofika mbele ya mfalme

Biblia ya Kiebrania inaweza pia kutasiriwa kwa kumaanisha, "Lakini Esta alipokuja mbele ya mfalme."

Esther 9:26

Purimu

Sikukuu iliyosherehekewa kukumbuza wokovu wa Wayahudi katika Uajemi kutoka kwa njama ya Hamani ya kuharibu na kuua Wayahudi wote ndani ya siku moja.

mbili

"2"

Siku hizi zilipawa kusherehekewa na kutunzwa

"Wayahudi walipaswa kusherehekea na kuzitunza siku hizi"

"wasikome kuzitunza kwa uaminifu"

"kutunza kwa uaminifu mara zote"

Esther 9:29

Abihaili

(Tazama: tafsiri ya majina)

barua ya pili

"barua ya nyongeza"

Esther 9:30

127

(Tazama: tafsiri ya namba)

majimbo

Tumia neno lile lile kama lilivyotumika katika 1:1.

walivyowaelekeza

"walijiweka"

sheria

mpangilio" au uendeshaji"

Esther 10

Esther 10:1

akaweka

"toza"

mafanikio

"yaliyotimizwa"

Esther 10:3

pili

"namba 2"

alitafuta

"taka" au "hitajika"

hali njema

"kuwa katika hali nzuri"

Job 1

Job 1:1

nchi ya Usi

Inawezekana maeneo haya ni 1) eneo katika Edomu mashariki ya mto Yordani mahali fulani magharibi ya Yordani ya sasa au 2) eneo mashariki ya mto Frati katika Irani ya sasa.

haki na mkamilifu

Neno "haki" na "mkamilifu" yana maana sawa na yanaeleza kwamba Ayubu alikuwa muadilifu. "Alitenda yaliyo mema mbele za Mungu."

mmoja aliyemcha Mungu

"mmoja aliyemheshimu Mungu"

kuepukana na uovu

Hapa uovu unazungumziwa kama vile eneo ambalo mtu ataepuka kwenda huko, badala ya kufanya matendo maovu. "alikataa kufanya uovu"

watoto saba wakiume na mabinti watatu

"wakiume 7 na mabinti 3"

Alimiliki kondoo elfu saba

"Alikuwa na kondoo 7,000"

ngamia elfu tatu

"ngamia 3,000"

jozi mia tano za maksai

"jozi 500 za maksai"

mkuu

"tajiri"

watu wote wa Mashariki

Inahusu maeneo yaliyokuwa mashariki ya Kanaani. "watu wote wanaoishi katika nchi zilizokuwa mashariki ya Kanaani"

Job 1:4

Kwa siku yake kila mtoto wa kiume, hufanya

Neno "siku" labda linahusu siku ambayo walisherehekea kuzaliwa kwa mtoto wa kiume. Lakini angalau inahusu wazo la kila mtoto wa kiume kuchukua mwelekeo katika kufanya sherehe. "Katika sherehe ya siku ya kila mtoto wa kiume, mwana hutoa" au " Kila mtoto wa kiume kwa upande wake hutoa"

hufanya ... Wakatuma ... Ayubu hutuma ... kuwatakasa ... Aliamka asubuhi na mapema ... na kusema

"kwa desturi alitoa ... kwa desturi walituma ... Ayubu kwa desturi alituma ... kwa desturi aliwaweka wakfu ... Kwa desturi aliamka mapema ... kwa desturi alisema"

yeye huwatakasa

Hapa "weka wakfu" humaanisha kumsihi Mungu kuondoa ibada yoyote chafu ambayo watoto wa Ayubu huenda waliileta juu yao wenyewe wakati wakisherekea kwa furaha pamoja. Ayubu alifanya haya kwa kuwatolea sadaka kwa Mungu.

pamoja nao

Neno "wao" linahusu watoto saba wa kiume na mabinti watatu lakini halimjumuishi Ayubu.

Baada ya siku za karamu zilipokuwa zimetimia

"Wakati sherehe zilipomalizika" au "Baada ya sherehe"

Ayubu hutuma kwao

"Kwa desturi Ayubu alituma mtu kuwaita waje kwake mwenyewe"

kumkufuru Mungu mioyoni mwao

Mara nyingi mawazo hayo huja bila kukusudia, bila mtu kusubiri kuyafikiri. "kumkufuru Mungu mawazoni mwao"

Job 1:6

siku ambayo

Hii haikuwa siku maalumu. Kusanyiko lilifanyika mara kwa mara. "wakati ambapo" au "siku moja wakati"

watoto wa Mungu

Hii inamaanisha malaika, viumbe wa mbinguni.

kujihudhurisha mbele za BWANA

"kusimama pamoja mbele za BWANA kama alivyo waagiza kufanya"

Natoka kuzunguka zunguka duniani, kutembea huku na huko humo

Msemo "kuzunguka zunguka" na "kutembea huku na huko" inakusudia kazi moja ya kusisitiza ukamilifu wake. "Kutoka mahali popote duniani."

BWANA

Hili ni jina la Mungu ambalo alilifunua kwa watu wake katika Agano la Kale. Tazama ukurasa wa tafsiri ya Neno Yahweh kuhusu namna ya kulitafsiri

kutembea huku na huko humo

"huku na huko" inahusian na kusafiri juu ya dunia yote.

Je umemwangalia mtumishi wangu Ayubu?

"Je umefikiri kuhusu mtumishi wangu Ayubu?" Hapa Mungu alianza kuzungumza na Shetani kuhusu Ayubu. "Angalia mtumishi wangu Ayubu"

mtu mwenye haki na mkamilifu

Neno "mwenye haki" na "mkamilifu" yana maana sawa na yanaeleza kwamba Ayubu alikuwa muadilifu. "Alitenda yaliyo mema mbele za Mungu."

mmoja aliyemcha Mungu na kuepukana na uovu

"mmoja aliyemheshimu Mungu" na "alikataa kufanya uovu." Hapa uovu unazungumziwa kama vile eneo ambalo mtu ataepuka kwenda huko, badala ya kufanya matendo maovu

Job 1:9

Je Ayubu amcha Mungu bila sababu?

"Je Ayubu anamheshimu Mungu bila sababu?" Shetani akamjibu Mungu kwa kuwasilisha na kujibu maswali yake mwenyewe. Akasema kwamba Ayubu anamheshimu Mungu tu kwa sababu Mungu anambariki yeye. "Ayubu ana sababu ya kumtii Mungu."

Wewe hukumwekea kinga pande zote, kuzunguka nyumba yake, na kuzunguka vitu vyote alivyo navyo kutoka kila upande

Shetani anaeleza ukweli kuunga mkono hoja yake. "Wewe umemlinda yeye, familia yake na kila kitu anachomiliki."

kumwekea kinga pande zote, kuzunguka nyumba yake

kama kizuizi kama vile ukuta au uwa wa miti iliyooteshwa kuzunguka na kulinda ardhi ya mtu, Mungu amemzungushia Ayubu na ulinzi wake. "akamlinda yeye na nyumba yake"

kazi za mikono yake

"Kila kitu ambacho anafanya"

mifugo yake imeongezeka katika nchi

"ana mifugo zaidi na zaidi katika nchi"

Lakini sasa nyosha mkono wako na uguse yote hayo aliyonayo, na uone kama hatakufuru mbele ya uso wako.

Shetani anamaanisha kwamba kama Mungu atamshambulia Ayubu, ataona namna ambavyo Ayubu atajibu. "Lakini sasa, kama utanyosha mkono wako na uguse vyote alivyonavyo, utaona atakavyo kufuru mbele ya uso wako"

Lakini sasa nyosha mkono wako

Hapa "mkono" unahusiana na uwezo wa Mungu wa kutenda. "Lakini sasa zitumie nguvu zako"

uguse yote hayo aliyonayo

Hapa "gusa" linawakilisha tendo la kudhuru au kuangamiza. "shambulia vyote alivyonavyo" au "angamiza vyote alivyonavyo"

ya uso wako.

Hii inahusu muda ambao Mungu yuko makini. "katika uwezo wake wa kusikia"

Tazama

"Tazama" au "kuwa makini na yote ambayo na kwenda kukuambia"

hayo yote aliyonayo yamo mkononi mwako

Hapa "mkono" unawakilisha uwezo wa mtu kudhibiti kitu fulani. "una uwezo juu ya yote aliyonayo."

juu yake yeye mwenyewe

"dhidi ya mwili wake" "lakini usimdhuru kimwili" au "usiudhuru mwili wake"

akatoka mbele za BWANA.

"aliondoka kutoka kwa BWANA" au "Akamwacha BWANA"

Job 1:13

Waseba

Hili lilikuwa eneo lililopo katika Yemeni ya siku hizi. Hapa linawakilisha kundi la wavamizi au wanyang'anyi kutoka Sheba.

wakawaangukia

Hapa "kuangukia" inawakilisha wazo la shambulizi. "wakawashambulia"

wamewaua

Hapa kushangaza inawakilisha mauaji.

makali ya upanga

Hapa "mdomo" unawakilisha sehemu ya jambia ambayo huua watu, ambayo ni, labda ncha au ukingo mkali. Pia, majambia yote ya watu kutoka Seba yaliongea kama vile walikuwa na jambia moja tu.

Job 1:16

Wakati alipokuwa akiendelea kusema

"yeye" linarejea mjumbe wa kwanza

akatokea mwingine

"mjumbe mwingine pia alifika"

Mimi pekee nimeokoka kukuletea habari.

Tafsiri kama katika 1: 13

Kwa wale watumishi, wamewaua kwa makali ya upanga. Mimi pekee nimeokoka kukuletea habari.

Tafsiri kama katika 1: 13

Job 1:18

Wana wako wa kiume na binti zako walikuwa wakila na kunywa mvinyo nyumbani mwa ndugu yao mkubwa

Tafsiri kama katika 1: 13

Upepo wenye nguvu

"kimbunga" au "dhoruba jangwani"

pembe nne za nyumba

"mihimili ya muundo wa nyumba"

Ikawaangukia vijana

"Nyumba ikawaangukia wana wako wa kiume na mabinti zako"

Mimi pekee nimeokoka kukuletea habari.

Tafsiri kama katika 1: 13

Job 1:20

akalirarua joho lake, akanyoa kichwa chake

Haya yalikuwa matendo ya taratibu za ibada ya maombolezo, kuashiria huzuni kumbwa.

Mimi nilitoka tumboni mwa mama yangu ni uchi, nami nitakuwa uchi wakati nitakaporudi huko

"Wakati wa kuzaliwa kwangu, si kuleta kitu duniani, na wakati wa kifo changu nitarudi udongoni bila kitu."

Katika mambo hayo yote

"Kuhusu haya yote yaliyotokea"

hakumwazia Mungu kwa uovu.

"kusema kwamba Mungu alifanya makosa"

Job 2

Job 2:1

Habari za jumla:

Mistari hii ipo sawa na 1: 6 na inawezekana kutafsiriwa katika namna moja.

Kisha kulikuwa na siku

Tafsiri kama katika 1: 6

siku ambayo

Hii haikuwa siku maalumu. Kusanyiko lilifanyika mara kwa mara. "wakati ambapo" au "wakati wa siku moja"

wana wa Mungu

Tafasiri kama katika 1: 6.

kujihudhurisha mbele za BWANA

Tafasiri kama katika 1: 6.

Natoka kuzunguka zunguka duniani, kutembea huku na huko humo.

tafasiri kama katika 1: 6.

Job 2:3

Habari za Jumla:

Mistari hii ipo sawa na 1: 6, isipokuwa kwa ongezeko la "Yeye anashikamana na utimilifu wake, japokuwa ulinichochea dhidi yake, nimwangamize pasipo sababu."

Je umemwangalia mtumishi wangu Ayubu?

Hili swali la kejeli kwa kweli inatengeneza maelezo. Tafasiri kama katika 1: 6. "Angalia mtumishi wangu Ayubu."

mtu mwenye haki na mkamilifu

Neno "haki" na "mkamilifu" yana maana sawa na yanaeleza kwamba Ayubu alikuwa muadilifu. "Alitenda yaliyo mema mbele za Mungu."

mmoja aliye mcha Mungu na kuepukana na uovu.

Hapa uovu unazungumziwa kama vile eneo ambalo mtu ataepuka kwenda huko, badala ya kufanya matendo maovu. "alikataa kufanya uovu" (Tafasiri kama katika 1: 1)

Hata sasa anashikamana na utimilifu wake

"amesalia amejitoa kikamilifu kufanya yale yaliyo ya haki na kweli"

ulinichochea juu yake

"ulinishawishi bila sababu nimshambulie"

nimwangamize

Hapa "angamiza" linawakilisha "kumfanya awe maskini." "kumfanya yeye awe mtu maskini"

Job 2:4

Ngozi kwa ngozi, hasa

"Ngozi" ni mfano wa maisha ya Ayubu. "Mtu atafanya chochote kuokoa maisha yake, hata kukubali kupoteza mali zake na wapendwa."

Lakini nyosha mkono wako sasa na uguse mifupa yake na nyama yake, na uone kama hatakufuru mbele ya uso wako.

Shetani anamaanisha kwamba kama Mungu atamshambulia Ayubu, yeye ataona namna Ayubu atakavyojibu. "Lakini sasa, kama utanyosha mkono wako na uguse mifupa yake na nyama yake, utaona utakavyokufuru mbele ya uso wako"

nyosha mkono wako

Hapa "mkono" unahusu uwezo wa Mungu kutenda. "Lakini sasa tumia nguvu zako." Tafsiri kama katika 1: 9.

gusa

Hapa "gusa" huwakilisha kitendo cha kudhuru. "shambulio"

mifupa yake na nyama yake

Maelezo haya yanawakilisha mwili wa Ayubu.

kufuru mbele ya uso wako

Tafasiri kama katika 1: 9.

uso wako

Hii inahusiana na wakati ambao Mungu yupo makini. "katika uwezo wako wa kusikia"

Job 2:7

Kisha Shetani akatoka mbele ya uso wa BWANA.

Tafasiri kama katika 1: 9.

akampiga

"kushambuliwa" au "athiriwa na"

majipu mabaya

makubwa, yanayowasha na maambukizi machungu ya ngozi

kipande cha kigae kujikunia

kusugua mikwaruzo ya ngozi ili kupunguza mwasho.

akaketi chini majivuni.

Hii yawezekana inahusiana na eneo ambalo takataka hutupwa na pengine huchomwa. kukaa katika eneo kama hilo ilikuwa alama ya maombolezo mazito. "kukaa kwenye rundo la takataka"

Job 2:9

Je hata sasa wewe unashikamana na utimilifu wako?

Hili swali la kejeli kwa kweli linatengeneza taarifa. Tafasiri kama katika 1: 6. "Angalia mtumishi wangu Ayubu."

Umkufuru Mungu

"Kumkataa Mungu"

unaongea kama mmoja wa hao wanawake wapumbavu

Ayubu akasema unaongea kama mwanamke mpumbavu. "Unaongea kana kwamba wewe ni mwanamke mpumbavu."

Je sisi tupate mema toka kwa Mungu na tusipate mabaya?

Swali hili la kejeli kwa kweli linawasilisha taarifa. "Bila shaka lazima tungelipata mabaya kutoka kwa Mungu pamoja na mazuri."

tupate mema

"kunufaika na mambo yote mazuri"

mema

Hili linawakilisha mambo yote mazuri ambayo Mungu hutupa.

tupate mabaya

"teseka na mateso yote mabaya bila kulalamika"

mabaya

Hili linawakilisha mambo yote mabaya ambayo Mungu hufanya au huruhusu ili sisi tupate maarifa.

tenda dhambi kwa midomo yake.

Hapa "midomo" inawakilisha tendo la kuongea. "dhambi kusema kwa kushindana na Mungu"

Job 2:11

Elifazi Mtemani, Bildadi Mshuhi, na Sofari Mnaamathi

Elifazi, Bildadi, na Sofari ni majina ya wanaume. Temani ulikuwa mji katika Edomu. Washuhi ni uzao wa Ibrahimu na Ketura (tazama Mwanzo 25: 1). Naamathi ulikuwa mji katika Kanaani.

Wakatenga muda

"walikubaliana juu ya wakati"

kuomboleza naye na kumfariji.

Hapa neno "omboleza" na "fariji" yana maana sawa. Rafikize wanajaribu kumfariji Ayubu na kuomboleza naye. "kuhuzunika na Ayubu ili kusaidia kupoza mateso yake."

Job 2:12

Walipoinua macho yao

"walikaza macho" au "walitazama kwa makini"

hawakuweza kumtambua

Hii yawezekana inamaanisha kwamba wageni wa Ayubu hawakuweza kumtambua kwanza, wakati walipo muona kwa mbali. Ayubu alionekana tofauti kuliko kawaida kwa sababu ya huzuni yake na kwa sababu ya kuwashwa mwili mzima. "kwa shida walimtambua"

Wakapaza sauti zao na kulia

"wakalia kwa sauti kubwa " au "wakalia sana"

akararua joho lake

Hii ilikuwa ishara ya maombolezo.

kurusha majivu hewani na juu ya kichwa chake

Hizi zilikuwa ishara za maombolezo.

Job 3

Job 3:1

akafunua kinywa chake

"alianza kusema"

Na ipotelee mbali siku niliyozaliwa mimi, usiku

Ayubu anaongea juu ya siku na usiku kana kwamba walikuwa watu. "Na tamani kwamba nisingekuwa nimezaliwa."

usiku uliosema, 'Mimba ya mtoto wa kiume imetungwa.'

kujieleza huku kunazidi maelezo ya huzuni ya Ayubu kwa kwenda wakati wa nyuma zaidi kutoka kuzaliwa kwake hadi kutungwa mimba yake. "usiku ambao ulisema, "Mtoto wa kiume amechukuliwa mimba' potevu."

usiku uliosema

Hapa usiku umeongelewa kana kwamba walikuwa watu ambao wanaweza kuongea. ... "usiku ule ambao watu walisema."

Mimba ya mtoto wa kiume imetungwa.'

Hii inaweza kuwekwa katika muundo hai. " mama yake amechukuwa mimba ya mtoto wa kiume."

Job 3:4

Habari za Jumla:

Semi zote katika mistari hii ni matamanio kwamba siku ya kuzaliwa kwake Ayubu isingekuwako tena. Hii inaweza husika na siku, japokuwa katika wakati uliopita, hata kuwepo kwa namna fulani. ... "Natamani kwamba siku nilipozaliwa ingelikuwa giza."

Siku hiyo na iwe giza ... wala mwanga usiiangazie

Vifungu hivi viwili vinaelezea giza la siku ya kuzaliwa kwake Ayubu, hivyo kurudia majuto ya Ayubu ya kuwa alikuwa amezaliwa.

Siku hiyo na iwe giza

Hili ni tamanio la kutokuwepo tena siku hiyo. "ikiwezekana siku hiyo itoweke."

Ishikwe na giza na kivuli la mauti liwe lake

Hapa giza na kivuli cha mauti vinazungumziwa kana kwamba ni watu ambao wanaweza kudai chochote kuwa ni mali yao. Neno "hii" inahusiana na siku ya kuzaliwa kwa Ayubu.

kivuli cha mauti

Hapa kivuli kinawakilisha mauti yenyewe. "kifo kama kivuli"

Wingu na likae juu yake

Hapa wingu linazungumziwa kana kwamba ni mtu ambaye anaweza kuishi juu ya siku ya kuzaliwa kwake Ayubu. "Ikiwezekana wingu liifunike hivyo hakuna mtu anayeweza kuiona"

kila kitu kiifanyacho siku kuwa giza

Hii inamaanisha vitu vizuiavyo nje mwanga wa jua na kutengeneza giza. Hapa "nyeusi" inawakilisha giza.

kiitishe

"itishe siku hiyo." Siku inazungumziwa kana kwamba ni mtu ambaye anaweza kutishwa na giza.

Job 3:6

na ukamatwe na giza tororo

Giza hili tena linazungumziwa kana kwamba ni mtu ambaye anaweza kuushika na kuuzuia usiku. "ikiwezekana giza nene kulifanya litoweke"

giza tororo

"giza sana" au "giza kabisa"

shangwe isiwe ndani yake.

Neno "hii" linahusiana na usiku wa kuzaliwa kwake Ayubu au mimba yake. Usiku wa mimba ya Ayubu unazungumziwa kana kwamba mtu ambaye hata kuwa na furaha. "Ikiwezekana usiku huo utoweke kwenye kalenda."

usiwekwe katika hesabu

Usiku huo unazungumziwa kana kwamba mtu ambaye anaweza kutembea. "ikiwezekana asiwepo mtu wa kuuweka katika hesabu"

usiku huo na uwe tasa

Usiku wa kuzaliwa kwake Ayubu unazungumziwa kana kwamba ni mwanamke. "ikiwezekana asizaliwe mtoto katika usiku huo"

sauti ya shangwe isiwe ndani yake.

Hapa usiku wa kuzaliwa kwake Ayubu unazungumziwa kana kwamba ni muda ambao ulikuwa bado unawezekana kwa mtu kuwa na furaha. "ikiwezekana asiwepo mtu wa kusikia kilio cha furaha wakati wa kuzaliwa mwana"

sauti ya shangwe kuja

Hapa sauti inasimama kwaajili ya mtu mwenye furaha. "Ikiwezekana asiwepo mtu wa kuwa na furaha katika hili milele"

Job 3:8

hao wafahamuo namna ya kumuamsha lewiathan

Hapa huenda Ayubu anamaanisha wachawi na waganga, ambao yeye anawaamini wanaweza kuwa na uwezo wa kumchochea Lewiathani katika kueneza machafuko. Lewiathani alikuwa mnyama bora aliyejulikana wakati wa Kale Karibu Mashariki ya mithiolojia, ambaye alifikiri kuwa dhamana kwa aina zote za uharibifu, maradhi, na machafuko.

Nyota za mapambazuko yake zitiwe giza

Hii inahusiana na sayari ambayo mara kwa mara huonekana sawasawa kabla ya mapambazuko. "Inawezekana nyota ambazo huonekana kabla ya siku hiyo kwanza mwanga uwe giza"

Siku hiyo iutafute mwanga, lakini isiupate

Siku ya kuzaliwa kwake Ayubu inazungumziwa kana kwamba ni mtu anayetazama kitu. "Inawezekana siku hiyo ilitarajia mwanga, lakini haikuupata."

wala makope ya mapambazuko isiyaone

Mapambazuko yanazungumziwa kana kwamba yana kope kama alizonazo mtu. "wala kuona mwanga wa kwanza wa mapambazuko."

kwasababu haikuifunga milango ya tumbo la mama yangu

Tumbo la uzazi la mwanamke linazungumziwa kana kwamba ni chombo chenye milango. "kwasababu siku hiyo haikulifunga tumbo la uzazi la mama yangu"

kwasababu haikunifichia taabu machoni pangu.

Siku ya kuzaliwa kwake Ayubu inazungumziwa kana kwamba ni ni mtu ambaye anaweza kuficha kitu.

machoni pangu.

Hapa "macho" yanawakilisha mtu ambaye anaonana nao. "kutoka kwangu"

Job 3:11

Habari za Jumla:

Kifungu hiki kina maswali manne ya kejeli, ambayo Ayubu anauliza ili kufanya mfululizo wa kweli wa maelezo.

Kwanini si-kufa wakati lipotokeza katika tumbo la uzazi?

"kwa nini sikufa wakati wa kuzaliwa?" Ayubu anauliza swali hili ili kulaani siku ya kuzaliwa kwake na kueleza majuto yake. "Natamani ningelikufa siku nilipozaliwa"

Kwanini sikuitoa roho yangu hapo mama aliponizaa?

Ayubu anamaanisha kusema kwamba yeye asingelizaliwa hai. "Natamani ningelikufa wakati nilipotoka nje ya tumbo la uzazi."

kuitoa roho yangu

Hii inahusiana na kifo.

kwanini magoti yake yalinipokea?

Labda hii inahusiana na paja la mama yake Ayubu. Magoti ya mama yake yamezungumziwa kana kwamba ni watu ambao wanaweza kumkaribisha mtoto mchanga. "Natamani kusingelikuwa na paja la kunipokea mimi."

Kwanini maziwa yake yanipokee hata ninyonye?

Maziwa ya mama yake Ayubu yanazungumziwa kana kwamba ni watu ambao wanaweza kumkaribisha mtoto mchanga. "Natamani kusingelikuwa na maziwa kwaajili ya kuninyoshesha."

Job 3:13

Kwa sasa ningelikuwa nimelala chini kimyakimya. Ningelala usingizi na kupata pumziko

Ayubu anatumia sentensi mbili kufikiri kuhusu ingelikuwaje kama yeye asingelizaliwa au angelikufa wakati wa kuzaliwa.

ningelikuwa nimelala chini kimya kimya

Ayubu anafikiria kitu ambacho kingeliweza kutokea katika siku za nyuma lakini hakikutokea, kama ilivyoelezwa hapo juu. "Ningelikuwa nimelala chini kimyakimya"

nimelala chini kimya

"lala, kupumzika kwa amani"

na kupata pumziko

Neno "pumziko" hapa linamaanisha kulala kwa amani, lakini pia huyo Ayubu asingelikuwa anapitia maumivu ambayo anayapata

pamoja na wafalme na washauri wa dunia,

"na wafalme na washauri wao"

Job 3:15

Habari za Jumla:

Ayubu anaendelea na fikira zake kuhusu kufa kabla ya kuzaliwa.

Au Ningelikuwa nimelala pamoja ... wasio uona mwanga kabisa.

Hii inaelezea kitu ambacho kingetokea lakini hakikuweza kutokea.

Au Ningelikuwa nimelala pamoja na wakuu

"Ningelikuwa nimepumzika na wakuu." Katika kifungu hiki, neno "lala" na "kupumzika" ni njia ya heshima kusema "haishi tena."

wenye dhahabu, waliozijaza nyumba zao fedha

Ayubu anatumia ulinganishaji kusisitiza kile anachosema.

Au pengine ningekuwa sijazaliwa, kama watoto wachanga wasio uona mwanga kabisa.

Ayubu anatumia ulinganishaji kusisitiza anachosema.

ningekuwa sijazaliwa

"Ningelikuwa nimekufa tumboni mwa mama yangu"

kama watoto wachanga wasio uona mwanga kabisa

"kama watoto wachanga ambao hawangelizaliwa"

watoto wachanga

"watoto" au "watoto wadogo sana"

Job 3:17

Habari za Jumla:

Ayubu anabadilisha mazungumzo yake kutoka kufa mpaka uzima baada ya kifo.

Huko waovu huacha kusumbua; huko waliochoka hupumzika.

Ayubu anatumia usambamba kusisitiza kuwa wanyonge watapata pumziko kutoka kwa wale walio wasababishia magumu.

Huko waovu huacha kusumbua

Ayubu anaongea kuhusu sehemu ambayo watu huenda baada ya wao kuacha kuishi. "Katika sehemu hiyo, watu waovu huacha kusumbua"

sauti ya msimamizi wa watumwa

Hapa "sauti" ni mfano wa nguvu ambayo msimamizi wa watumwa anakuwa nayo juu ya watumwa. "Hawako tena chini ya udhibiti wa watumwa"

wadogo na watu maarufu

Hii ni tamathali ya usemi ambayo humaanisha "watu wote, watu masikini na watu matajiri."

mtumishi yuko huru kwa bwana wake huko.

Mtumishi hana wajibu wa kumtumikia bwana wake.

Job 3:20

Kwa nini yeye aliye mashakani kupewa mwanga? Kwa nini hao wenye uchungu moyoni kupewa uhai

Maswali mawili ya Ayubu kimsingi humaanisha kitu kimoja. Yeye anashangaa kwanini hao ambao hukabili magumu huendelea kuishi.

Kwa nini yeye aliye mashakani kupewa mwanga?

Hapa Ayubu anashangaa kwanini lazima watu wabaki hai na kuteseka. "Mimi sielewi kwa nini Mungu hutoa uhai kwa mtu ambaye anateseka"

mwanga

Hapa mwanga unawakilisha uhai

Kwa nini hao wenye uchungu moyoni kupewa uhai ... hazina iliyofichika?

"je kwa nini Mungu hutoa uhai kwa mtu mwenye taabu? "Mimi sielewi kwa nini Mungu anatoa uhai kwa mtu mwenye huzuni sana ... hazina iliyofichika"

ambao hutamani mauti lakini hawapati

Hapa kifo kinazungumziwa kana kwamba kuna kitu kinakuja kikimwelekea mtu fulani. "kwa mtu ambaye haitaji tena kuwa hai, lakini bado yu-hai"

ambao huyachimbulia mauti zaidi ya kutafuta hazina iliyofichika

Mtu anayetumainia kufa anazumgumziwa hapa kana kwamba anachimbua hazina iliyozikwa. "kwa mtu ambaye anahitaji kufa zaidi ya yeye kutafuta hazina iliyofichika"

Kwa nini kupewa mwanga ambao hushangilia mno na kufurahi walionapo kaburi

Hapa Ayubu anatumia swali kufanya kauli. "Mimi sielewi kwa nini Mungu anaruhusu mtu kuendelea kuishi wakati mtu huyo angefurahi kuzikwa katika udongo"

ambao hushangilia mno na kufurahi

Msemo wa "hufurahia sana" kimsingi unamaanisha kitu kimoja kama "furaha." Pamoja, misemo yote miwili inatilia mkazo wa nguvu ya furaha. "mtu ambaye ana furaha sana"

alionapo kaburi

Hii ni njia ya heshima ya kumaanisha kufa. "wakati yeye akifa na anaweza kuzikwa"

kaburi

Hapa kaburi linawakilisha kifo.

Job 3:23

Kwanini kupewa mwanga mtu ambaye njia zake zimefichika, mtu ambaye Mungu amemzungushia uwa?

Ayubu anauliza hili swali ili kutengeneza habari. "Mungu hatoi uhai kwa mtu na kisha kuzichukua mbali siku zake za baadaye na kumwekea mpaka yeye."

Kwanini kupewa mwanga mtu

Hapa mwanga unawakilisha uhai. "Je kwa nini Mungu humweka mtu hai"

ambaye njia zake zimefichika

Hapa Ayubu anaongelea siku zake za baadaye, ambazo yeye hazijui mapema, kana kwamba Mungu alikuwa amezificha kutoka kwake.

mtu ambaye Mungu amemzungushia uwa

Hapa kuwa katika matatizo na hatari yanasemwa kana kwamba walikuwa wamefungwa ndani ya mipaka finyu.

kushusha kwangu pumzi kwatokea badala ya kula; kuugua kwangu kumemiminika kama maji

Ayubu anaelezea maumivu yake makubwa katika njia mbili.

kushusha kwangu pumzi kwatokea badala ya kula

"Badala ya kula, mimi naomboleza"

kuugua kwangu kumemiminika kama maji.

ubora wa maadili na hisia kama vile huzuni mara kwa mara huongelewa kana kwamba yalikuwa maji.

Job 3:25

jambo lile niliogopalo limenipata; nalo linitialo hofu limenijilia

misemo hii miwili ina maana moja. "kile nikiogopacho sana kimenitokea mimi" au "liniogopeshalo vibaya sana limenijilia kweli.

Mimi sioni raha, sipati utulivu, na sipati pumziko;

Ayubu anaelezea maumivu yake katika misemo mitatu inayotenganishwa. "Nina mashaka sana" au "mimi nimeteseka kihisia na kimwili

badala yake huja taabu

Taabu imezungumziwa kana kwamba lilikuwa jambo ambalo lingeweza kumwijia Ayubu. "badala yake msiba unanitesa mimi"

Job 4

Job 4:1

Elifazi

Elifazi ni jina kiume.

Mtemani

Mtemani ni mtu wa kabila la Temani.

je utakosa ustahimilivu?

Elifazi anauliza swali hili ili kutengeneza maelezo. "wewe kweli utakosa uvumilivu."

je utakosa ustahimilivu?

"Hicho kitakukera wewe?"

ni nani anaweza kujizuia asizungumze?

Elifazi anauliza swali hili kusema kwamba hakuna mtu ambaye amuonaye rafiki yake anateseka akakaa kimya. "Hakuna mtu awezaye kujizuia mwenyewe kuongea (kwa rafiki yake katika hali hiyo kama uliyonayo wewe mwenyewe)" au "Mimi lazima nizungumze na wewe, (kwa kukuona kuwa upo katika hali ya majonzi)."

Tazama, wewe umewafunza wengi; wewe imeipa nguvu mikono iliyokuwa dhaifu.

Mstari huu unaeleza wazo moja katika njia mbili tofauti.

umeipa nguvu mikono iliyo dhaifu.

Hapa "mikono dhaifu" inawakilisha watu ambao wanahitaji msaada. "wewe uliwasaidia wengine wakati walipohitaji msaada"

Job 4:4

Habari za Jumla:

Mwandishi anatumia ulinganishaji katika kila mistari hii kutengeneza wazo moja akitumia habari mbili tofauti kusisitiza 1) kuunga mkono kwamba Ayubu aliwasaidia wengine siku zilizopita, 2) madhara juu yake kwa taabu zake za sasa, na 3) unyenyekevu wake mbele za Mungu.

yamemsaidia

mtu fulani ambaye alishawahi kutiwa moyo anazungumziwa kana kwamba yeye alishikwa asianguke chini.

umeyaimarisha magoti dhaifu

Hapa kukatisha tamaa kunazungumziwa kana kwamba ni mtu ambaye magoti dhaifu hayawezi kumweka yeye wima.

Lakini sasa matatizo yamekuja kwako

Hapa matatizo yanazumziwa kana kwamba ni jambo ambalo linaweza kumfika mtu. "Lakini sasa wewe unateseka na masaibu"

wewe umechoka

"umekata tamaa"

hofu yako

"ni kweli kwamba una mweshimu Mungu"

Je si hofu yako imani yako, na ukamilifu wa njia zako tumaini lako?

Elifazi anauliza maswali haya ili kutengeneza usemi kwa Ayubu kwamba dhambi zake zimemsababishia yeye kuteseka. "Kila mmoja anafikiri kwamba unamheshimu Mungu; kila mmoja anafikiri kwamba wewe ni mtu mwaminifu. Lakini mambo haya lazima hayawezi kuwa kweli, kwa sababu wewe humwamini Mungu tena."

hofu yako

Elifazi anamaanisha hofu ya Ayubu kwa Mungu. "hofu yako kwa Mungu"

njia zako

Hapa "njia zako" inawakilisha "mwenendo wako," "namna unavyoenenda."

Job 4:7

ni nani aliyeangamia akiwa hana kosa?

Elifazi anatumia swali hili kumshawishi Ayubu kuchunguza dhambi katika maisha yake (na hukumu takatifu ya Mungu) kama kisababishi cha yeye kupotea. "Hapa mmoja aliyeangamizwa wakati hana kosa."

ni lini watu wakamilifu walikatiliwa mbali

Swali hili pia linamaanisha kutengeneza maelezo, na yanaweza kuwekwa katika umbo la kufaa. "Hakuna hata mmoja aliyewahi kumkatilia mbali mtu mkamilifu."

katiliwa mbali

Hapa kukatiliwa mbali inamaanisha kuangamizwa.

walimao uovu ... kupanda taabu ... huvuna

Hapa matendo ya kulima na kupanda yanawakilisha kinacho sababisha taabu kwa watu wengine. Tendo la kuvuna ni mfano wa mateso ya taabu ambazo mtu huzisababisha mwenyewe.

Kwa pumzi ya Mungu huangamia; kwa mlipuko wa hasira zake huteketea

Mwandishi anaeleza wazo moja akitumia taarifa mbili tofauti. Huu ni muundo wa ushairi wa kiebrania utumikao kwa kusisitiza, udhahiri, mafundisho, au yote matatu.

pumzi ya Mungu

Hii inaweza kuwa mfano wa tendo la Mungu la kutoa amri.

mlipuko wa hasira

Usemi huu unaashiria upumuaji mkubwa ambao mtu wakati fulani huufanya kupitia pua zake wakati akiwa na hasira.

pumzi ... mlipuko

msemo wa pili umejengwa juu ya wa kwanza. Zinaunda wazo moja kwa kutumia maana ambazo zinaongeza matokeo. "Kwa mpumuo wa mdomo wa Mungu wanafariki; mwendo kasi wa upepo wa hasira zake huwateketeza wao."

huangamia ... huteketea.

Fungu la pili limejengwa juu ya la pili. Yanaunda wazo moja. "Kwa mpumuo wa mdomo wa Mungu wanafariki; mwendo kasi wa upepo wa hasira zake huwateketeza wao."

huteketea.

Hapa kuteketezwa au kuliwa ni mfano wa kuuliwa.

Job 4:10

Habari za Jumla:

Mwandishi anatumia ulinganishaji katika mistari hii, anawasilisha wazo moja akitumia maelezo tofauti kutilia mkazo uharibifu wa Mungu kwa watu waovu.

Kuunguruma kwa simba, sauti ya simba mkali, meno ya simba wadogo - yamevunjika.

Hapa muungurumo wa simba, sauti yake, na meno yake yamevunjika vinatumika kama mfano wa kuangamizwa kwa waovu.

yamevunjika

Hii inaweza kuwekwa katika umbo halisi. "kitu fulani kimeyavunja"

Simba mzee huangamia kwa kukosa wahanga; watoto wa simba jike wametawanyiko kila mahali

Elifazi anatumia picha ya simba mzee anayekufa kwa njaa na familia yake imetawanyika kama sitiari ya kuangamizwa kwa waovu

wametawanyika

"kitu fulani kimetawanya watoto wa simba"

Job 4:12

Sasa nililetewa kwangu jambo fulani kisiri ... sikio langu likapokea uvumi kuhusu hilo

vifungu hivi vinaelezea wazo sawa katika njia tofauti. Vinawasilisha wazo kuwa Elifazi amesikia ujumbe uvumao kwake. Urudiaji huu ni muundo wa ushairi wa kiebrania umetumika mara kwa mara kwa kusisitiza, kufundisha, au udhahiri.

nililetewa kwangu jambo fulani kisiri

"kitu fulani kimeleta kwangu jambo fulani kwa siri"

maono wakati wa usiku

"ndoto"

wakati uwaangukiwapo usingizi mzito watu

"wakati watu wakisinzia sana"

Job 4:14

Habari za Jumla:

Mwandishi anatumia ulinganishaji katika mistari hii, kuwasilisha wazo moja akitumia maelezo tofauti kusisitiza hofu ya Elifazi.

nilipopatwa hofu na kutetemeka

Hapa hofu na kutetemeka yanazungumziwa kana kwamba ni mambo ambayo yanaweza kumwijilia mtu. "Mimi nikanza kuogopa na kutetemeka."

nywele zangu za mwili zilisimama

Hii inaonyesha hofu kubwa.

nywele za mwili wangu

"Nywele juu ya mwili wangu"

Job 4:16

Habari za Jumla:

Mwandishi anatumia ulinganishaji katika mstari wa 17, kuwasilisha wazo moja akitumia maelezo mawili tofauti kutilia mkazo swali kuhusu utakatifu wa mwanadamu mbele za Mungu.

Umbo lilikuwa mbele ya macho yangu

"Kitu fulani kilikuwa mbele ya macho yangu," "nimeona kitu fulani"

nami nikasikia

"Kisha nikasikia"

Je binadamu mwenye kufa anaweza kuwa mwenye haki zaidi kuliko Mungu?

Elifazi anatoa swali hili ili kwamba Ayubu akumbuke, "Naweza kujiangalia mimi mwenyewe kama mwenye haki zaidi ya Mungu?" au "Je nimethibitika mbele za Mungu?" "Binadamu mwenye kufa hawezi kuwa mwenye haki zaidi ya Mungu" au "Binadamu mwenye kufa hawezi kuwa mwenye haki mbele za Mungu."

Je mtu anaweza kuwa msafi zaidi kuliko Muumba wake?

Swali hili lina lengo sawa kama swali lililotangulia. "Binadamu hawezi kuwa msafi zaidi kuliko Muumba wake."

Muumba

"Mfanyaji"

Job 4:18

wale waishio katika nyumba za udongo, ambao misingi yao ipo katika vumbi

Huu ni utumiaji wa lugha ya picha kumwelezea mtu, ambaye aliumbwa kutokana na vumbi la udongo na ambao miili yao iko kama nyumba, ambazo zimejengwa kwa udongo na kuwa na misingi mibovu.

hupondwa mapema kuliko nondo

Kirai "mapema zaidi" kwa kawaida inatafasiriwa kama "kabla." "hupondwa kabla ya nondo" au " hupondwa sawa na nondo"

wameangamizwa

"kitu fulani kinawaangamiza wao"

wameangamizwa

"wameuawa"

Job 4:20

Habari za Jumla:

Mistari hii inaendeleza matumizi ya awali ya ulinganishaji, hapa inasisitiza katika njia tofauti wazo kwamba watu hufa ghafla pasipo kupata hekima na wala usumbufu kutoka kwa wengine.

Kati ya asubuhi na jioni wameangamizwa

Hii inamaanisha wazo la kitu fulani kinachotokea upesi.

wameangamizwa

Hii pia inaweza kuwekwa katika umbo hai. "wamekufa"

Je kamba za hema yao hazikung'olewa kati yao?

Hii inaweza kuwekwa katika umbo hai. "Si adui zao waliong'oa kamba za hema zao kutoka miongoni mwao?"

kamba za hema yao

Hapa kamba za hema zinawakilisha hema. Wakati mwingine nyumba ya mtu na familia zinafananishwa kama hema yake, ambayo inaweza pia kuwakilisha mali zake zote.

Job 5

Job 5:1

Utamrudia yupi katika watakatifu hao?

Elifazi anatoa swali hili kutengeneza hoja kuwa hakuna hata mmoja Ayubu anaweza kumgeukia kwa ajili ya msaada. "Je kuna mtakatifu yeyote ambaye unaweza kumgeukia?" au "Hakuna mtakatifu yeyote ambaye unaweza kumgeukia kwa ajili ya msaada."

watakatifu

Hii imaanisha viumbe bora kwa asili katika baadhi ya tabia, kama malaika au roho zingine

mjinga ... mtu mpumbavu

Hii inahusiana na mtu yeyote mjinga na mtu yeyote mpuuzi.

wivu huua mjinga

"wivu huua yeyote ambaye anatenda kijinga na maamuzi ya ghafla"

mtu mpumbavu akishika mzizi

Hapa mtu anazungumziwa kana kwamba ni mmea, huenda anakuwa mpuuzi zaidi kadri muda unavyosogea. "mtu mpuuzi anakuwa amejengwa katika ujinga zaidi"

makazi yake

Hii inahusiana na familia ya mtu na mali zake zote.

Job 5:4

Habari za Jumla:

Mistari hii inaendeleza matumizi ya awali ya ulinganishaji, hapa inatilia mkazo katika njia tofauti wazo kwamba watoto wa watu wajinga hawapo salama.

Watoto wake wako mbali na uzima

"yake" inahusiana na mtu mjinga au watu wajinga katika 5:1. "Watoto wao si salama milele"

wameangamia

Hapa kuangamizwa ni mfano wa kuonewa, kutumiwa vibaya, katika mahakama. Wazo hili linaweza kuwekwa katika umbo hai. "mtu fulani amewaangamiza"

lango la mji.

Lango la mji, linafanya kazi kama mahakama, ilikuwa sehemu ambayo ugomvi uliamuliwa na hukumu kutolewa.

Hakuna yeyote atakaye waponya.

"Hakuna yeyote wakuwaokoa watoto wa watu wapuuzi kutoka kwenye dhiki zao"

hata huyachukua katikati ya miiba

Inawezekana huu ni mfano wa kipande cha shamba ambapo mazao mabaya sana humea, kwasababu ya uwepo wa mimea yenye miba.

Wenye kiu huzitaka sana mali zao

Hapa watu waroho wanaongelewa kana kwamba wanakiu, na utajiri wa mtu mpumbavu unazungumziwa kana kwamba ni kitu fulani ambacho wanaweza kunywa.

Job 5:6

Kwa kuwa magumu hayatoki udongoni; wala taabu haichipuki katika nchi

Hapa magumu na taabu yanazungumziwa kana kwamba ni mimea.

wanadamu huzaliwa kwaajili ya taabu, kama cheche za moto zirukavyo juu.

Ni kama asili ya watu, mara tu wazaliwapo, kuwa na taabu kama ilivyo kwa cheche za moto zirukavyo juu.

Job 5:8

Habari za Jumla:

Katika mistari hii, Elifazi anaendeleza hotuba toka 4: 1. Mwandishi anaenedelea kutumia ulinganishaji katika kila mstari, kuwasilisha wazo moja akitumia maelezo mawili tofauti kusisitiza kwamba Ayubu lazima akiri hali yake kwa Mungu ambaye hutenda mambo ya kustajabisha.

makuu na mambo yasiyochunguzika, mambo ya ajabu yasiyo na hesabu

"Mambo makuu ambayo hayawezi fahamika, maajabu ambayo hayahesabiki"

mambo yasiyochunguzika

Hii inamaanisha mambo ambayo wanadamu hawezi kuyaelewa.

makuu na mambo yasiyochunguzika

Hapa mwandishi anatumia maneno mawili yanayojitegemea na kuunganishwa kwa "na" kusisitiza ukuu wa matendo ya Mungu. "mambo makuu sana yenye kuhitaji maarifa mengi"

mambo ya ajabu

"mambo ya kustajabisha" au "maajabu"

Job 5:11

Habari za Jumla:

Mwandishi anaendelea kutumia ulinganishaji katika kila mstari, kuwasilisha wazo moja akitumia maelezo mawili tofauti kusisitiza namna Mungu anavyo wainua wale ambao ni wanyonge na kuwashusha wale ambao ni werevu.

Hufanya haya kwaajili ya kuwainua juu hao walio chini

Watu wanyenyekevu wakati wa dhiki wanazungumziwa kana kwamba wako katika nafasi ya chini. Wakati Mungu akiwaokoa, wanapokea heshima. wakati hili likitendeka, wanazungumziwa kuwa kama wamepandishwa juu na kuweka katika nafasi ya juu. "Mungu hufanya hili ili kuwaokoa na kuwaheshimu wanyenyekevu ambao wamekuwa wakitaabika"

Yeye huharibu mipango

Hapa kuzuia mipango ya watu mwenye hila inazungumziwa kana kwamba ni vitu ambavyo vinaweza kuharibika kihalisia.

Yeye huwanasa watu wenye hekima katika matendo ya hila zao wenyewe

Hapa kuwafanya watu wenye hekima wataabike kwasababu ya matendo yao maovu inazungumziwa kana kwamba wamekamatwa katika mitego. Matendo yao wenyewe yanazungumziwa kana kwamba ni ile mitego.

watu waliogeuzwa

Hapa kuwa muovu kwa njia ya akili inazungumziwa kana kwamba umegeuzwa. "wale ambao ni werevu" au "wale ambao ni wajanja" au "wale ambao makini"

Job 5:14

Habari za Jumla:

Mwandishi anaendelea kutumia ulinganishaji katika kila mstari, kuwasilisha wazo moja akitumia taarifa mbili tofauti kusisitiza namna Mungu anavyowashusha wale ambao ni werevu na kuwaokoa wale ambao ni masikini.

hupatwa na giza wakati wa mchana

Hapa mwerevu, watu waovu ambao Mungu amewachanganya wanazungumziwa kana kwamba bila matarajio wakawa gizani wakati wa adhuhuri, wakati jua likiwa sehemu ya katikati ya anga. Hawawezi kufanya chochote wanachotamani kufanya, kwasababu hawawezi kuona. "Wale ambao ni werevu wako gizani, hata wakati wa muda wa adhuhuri"

kupapasa

papasa kwa mikono pande zote kama mtu kipofu

wakati wa mchana

"saa sita mchana"

Lakini yeye huokoa maskini kwa upanga wa vinywa vyao

Hapa mambo ya matusi na vitisho ambayo watu husema yanazungumziwa kana kwamba ni upanga vinywani vyao. "Lakini humwokoa mtu masikini kutokana na vitisho vya mwenye uwezo" au "Lakini yeye humwokoa mtu masikini wakati mwenye uwezo anapowatisha au kuwatukana wao"

udhalimu hufumba kinywa chake mwenyewe.

Watu ambao husema mambo yasiyo haki wanazungumziwa kana kwamba wao ni wadhalimu, ambao lazima waache kuongea. "Hata hivyo ni kama mdhalimu afunge mdomo wake."

Job 5:17

Habari za Jumla:

Mwandishi anaendelea kutumia ulinganishaji katika mstari wa 18 na 19, kuwasilisha wazo moja akitumia maelezo mawili tofauti kusisitiza matendo ya Mungu ya kuongoza na kuponya.

kutiwa adabu na Mungu ... uongozi wa Mwenyezi

Mungu ni mfano wa mzazi atiavyo adabu au aelekezavyo mtoto.

amebarikiwa

"umependelewa"

usidharau

"usikatae au " au "usiwangalie wasio na thamani"

uongozi

"mafunzo" au "ukusanyaji" au "adilisha"

Kwa kuwa yeye hujeruhi na kisha huuguza; yeye hutia jeraha na kisha mikono yake huponya

"kwa kuwa yeye hujeruhi lakini hufunga zaidi; yeye huangamiza lakini mikono yake huponya"

mikono yake huponya

Hapa "mikono yake" ni mfano wa Mungu.

Yeye atakuokoa na mateso sita; kweli, katika mateso saba, hakuna uovu utakao kugusa

matumizi ya ongezeko la hesabu kama vile "sita" na "saba" ni mfano wa wazo la wengi, mara nyingi. "Yeye atakuokoa kutoka katika taabu zaidi na zaidi; kwa kweli, muda baada ya muda, hakuna uovu utakao kugusa wewe"

Job 5:20

Habari za Jumla:

Mabadiliko katika kiwakilishi kutoka (yeye" hadi "wewe" ambayo yalianzia katika 5:17 yanaendelea hadi mwisho wa usemi ya Elifasi katika 5: 26.

Wakati wa njaa atakukomboa

"wakati wa njaa Mungu atakuokoa wewe"

atakukomboa wewe

"atakukomboa wewe" au "atakuokoa wewe" au "atakunusuru"

uharibifu

"madhara kutoka kwa maadui"

hutatishika na wanyama mwitu

"wewe hutaogopa wanyama mwitu"

wanyama mwitu

wanyama ambao hawajafugwa au hawajafundishwa.

Job 5:23

Habari za Jumla:

Mwandishi anaendelea kutumia ulinganishaji katika kila mistari hii, akiwakilisha wazo moja kwa kutumia maelezo mawili tofauti kusisitiza usalama na kuhusu ulimwengu wa asili, nyumba ndani ya shamba, na vizazi vya mmoja.

utakuwa na mapatano na mawe ya shambani mwako

Sentensi hii inatumia lugha ya picha kuwasilisha ulingalifu na ulimwengu wa asili. "mapatano yako na mawe ya shambani"

wewe utakuwa na amani na wanyama wa mwituni

"wanyama mwitu watakuwa na amani na wewe"

wanyama wa mwituni

Wanyama ambao hawajawahi kufungwa au kufundishwa

utajua kwamba hema lako lina usalama

"utafahamu kwamba hema lako lina amani"

utatembelea zizi la kondoo wako na hutakosa kitu chochote

"wewe utatembelea kundi lako na kukuta hakuna kilichopotea"

Pia utafahamu kwamba uzao wako utakuwa mwingi, na vizazi vyako vitakuwa kama nyasi juu ya ardhi

Katika usemi huu, "kizazi" ni mfano wingi sana kama bapa la majani. "pia wewe utafahamu kwamba uzao wako utakuwa mwingi, kwamba kizazi chako kitakuwa kama majani juu ya ardhi"

Job 5:26

Wewe utafika kaburini kwako mwenye umri kamili

"wewe utakufa katika umri wa uzee sana"

kama vile rundo la mashuke ya nafaka ambalo limembebwa juu kupelekwa kwenye uwanja wa kupuria

Elifazi anatumia ulinganifu kutengeneza wazo lake kwamba Ayubu atakufa wakati muda wake wa kufa ukifika. "Kama tu nafaka zivunwavyo kwa wakati, hivyo wewe utakufa wakati wako ukifika."

Tazama, tumelipeleleza jambo hili; ndivyo lilivyo; lisikie, na ulifahamu kwa ajili yako mwenyewe.

"Sisi" inamhusu rafiki zake Ayubu, akiwemo Elifazi, amabaye anazungumza. "Tazama, Sisi tumefikiri kuhusu jambo hili. Sikiliza kile ninsema na ufahamu kwamba ni kweli."

Job 6

Job 6:1

laiti maumivu yangu makubwa yangepimwa; laiti misiba yangu yote mikubwa ingewekwa kwenye mizani!

Hapa mwandishi anatumia maelezo mawili tofauti kuwasilisha wazo moja, mzigo wa mateso ya Ayubu.

kwenye mizani

"kwenye kipimo"

Kwa kuwa sasa ungekuwa mzito kuliko mchanga wa baharini

Ayubu analinganisha mzigo wa mateso yake na uzito wa mchanga wenye majimaji; vyote vinaweza kumwangamiza mtu. "Mzingo wa maumivu yangu makubwa na taabu ni mazito kuliko mchanga wa ufukweni."

Job 6:4

Habari za Jumla:

Mwandishi anaendelea kutumia ulinganishaji katika kila moja ya mistari hii, akiwasilisha wazo moja akitumia maelezo mawili tofauti kusisitiza maumivu makali sana ya Ayubu kama sababu ya malalamiko yake.

Kwa kuwa vitisho vya Mungu vimejipanga vyenyewe dhidi yangu

Huu ni ulinganishi wa mateso ya Ayubu. Yeye analinganisha taabu zake nyingi na mishale ambayo choma mwili wake.

moyo wangu umelewa sumu

Ulinganishaji unaendelea. Maumivu yamepenya hadi moyoni mwa Ayubu. "Nasikia maumivu ndani ya moyo wangu."

Vitisho vya Mungu vimejipanga vyenyewe dhidi yangu

"mambo yote mabaya sana ambayo yameweza kutokea dhidi yangu yamekuja kwa wakati mmoja."

kwa mishale

"kama kikosi cha jeshi chini ya kanali" u "kama kundi la wanajeshi"

Je punda mwitu hulia akiwa na malisho? Au ng'ombe huwa dhaifu wakati wa njaa ambapo anachakula?

Ayubu anatoa maswali haya kusisitiza kwamba ana maana nzuri kulalamika. " Tafadhari mimi ningelilalamika kama kila kitu kipo vizuri?" au "Tafadhari mimi nisingelilalamika bila sababu."

mlio

ni sauti aitoayo punda

dhaifu

sauti aitoayo ng'ombe

chakula

chakula cha mifugo

Je inawezekana kitu kisicho na ladha kulika bila chumvi? Au kuna radha yoyote katika ute mweupe wa yai?

Hata chakula, au hali ya mambo, katika maisha ya Ayubu ni ya kuhuzunisha. Ayubu analinganisha maisha yake na mlo ambao hauna viungo au ladha. "Maisha yangu hayana mwokoaji; ni kama ute mweupe wa yai usio na ladha."

Je inawezekana kitu kisicho na ladha kulika

Swali hili la kutoonyesha hisia linaweza kutafasiriwa kama maelezo hai: "Mtu hawezi kula chakula chenye ladha mbaya bil chumvi."

Job 6:7

Habari ya Jumla:

Mwandishi anaendelea kutumia ulinganishaji katika kila mistari hii, kuwasilisha wazo moja akitumia maelezo mawili tofauti kusisitiza mateso yake makali sana na haja yake ya kufa.

Nakataa kuvigusa

"Wao" inahusu chakula chenye ladha mbaya. Hapa Ayubu anaendelea kutumia sura ya chakula kibaya kama sitiari kwa hali ya mambo yasiyokubalika.

Oo, kama nigeweza kupata haja yangu; oo, kama Mungu angeridhia jambo nilitamanilo sana

"Oo kwamba Mungu angefanya kile ambacho nimemwomba yeye kufanya"

kama Mungu ingempendeza kuniangamiza mara moja

"Kwamba Mungu angelisonga mbele na kuniangamiza mimi"

kwamba angeulegeza mkono wake na kuyakatilia mbali maisha yangu

"kwamba angelitenda haraka na kufupisha maisha yangu"

angeulegeza mkono wake

"tenda haraka"

Job 6:10

Hii inaweza kuwa faraja yangu hata sasa

"Hata hivyo hii inaweza kuwa faraja yangu" au "Hii inaweza kuniletea faraja"

hata kama nafurahia sana maumivu ambayo hayapungui

"Mimi nita ruka kwa furaha katika maumivu yasiyokwisha" au "Mimi nitavumilia maumivu ambayo hayapungui"

nafurahia sana

"furahi"

yasiyopungua

"hayapungui"

kwa kuwa sikuyakana maneno yake Mtakatifu

"hivyo sikumkana Mungu"

Nguvu yangu ni ipi, hata nijaribu kusubiri? Mwisho wangu ni upi, utakao refusha maisha yangu?

Ayubu anatoa maswali haya kusisitiza kwamba hakuna maana ya yeye kuendelea kuishi. "Zaidi, kuna nini tena kipo kwaajili yangu kuishi na kukitumainia?" au "Mimi sina nguvu za kuendelea kuishi; Mimi sina sababu ya kuwa mstahamilivu"

Job 6:12

Habari ya Jumla:

Mwandishi anatumia maswali ulinganishi ya kejeli katika kila mistari hii, akiwasilisha wazo moja kutumia maelezo mawili tofauti kusisitiza ukosefu wa nguvu za kustahamili mateso.

Je nguvu zangu ni nguvu za mawe? Au mwili wangu umeumbwa kwa shaba nyeusi?

Ayubu analinganisha udhaifu wa mwili wake na ugumu, vifaa vya ujenzi vya kudumu sana kusisitiza ukosefu wake wa nguvu. "Mimi siko imara kama mawe. Mwili wangu hujaumbwa kwa kokoto za kutengenezea barabara."

Je si kweli kwamba sina msaada ndani yangu ... nami?

"Ni kweli kwamba sinanguvu zilizobaki ... mimi."

hekima imeondolewa mbali nami?

"mafanikio yangu yameondolewa kwangu" au "au "nguvu za ndani zimeondolewa kwangu" Hii inaweza kutajwa katika muundo hai. "Nguvu zangu za ndani zienda."

Job 6:14

Kwa mtu ambaye yu karibu kuzirai, inapasa uaminifu uonyeshwe na rafiki zake

"Rafiki anatakiwa kuwa na huruma kwa mtu ambaye anajihisi kukata tamaa"

hata kwake yeye aachaye kumcha Mwenyezi

"hata kama ataacha kumweshimu Mwenyezi Mungu" Maana za kufaa ni 1) mtu hana hofu ya Mungu au 2) rafiki zake hawamwogopi Mungu.

Lakini ndugu zangu wamekuwa waaminifu kwangu kama mkondo wa maji jangwani

Ayubu anawaelezea rafiki zake kuwa wamekuwa kama "bondejangwa" ambalo hupitiwa na mto katikati yake ambao unaweza kukauka ghafra na si wa kutumainika.

mfano wa mifereji ya maji ipitayo mpaka pasipo kitu

"mfano wa mito ya maji ambayo hukauka"

ambayo imetiwa giza kwa sababu ya barafu juu yake

"ambayo ni giza kama barafu"

na kwa sababu ya theluji ambayo hujificha yenyewe ndani yake

"na theluji hujificha ndani yake" au "barafu hupotea ndani yake"

Wakati zikiyeyuka, hutoweka

"Wakati zikipata joto, hutoweka"

kukiwa na joto, hutoweka mahali hapo.

"wakati wa joto, hukauka"

Job 6:18

Misafara ambayo husafiri kwa njia hiyo hugeuka kwaajili ya maji

Ayubu anaendelea na maelezo yake kuhusu rafiki zake kuwa si wa kutegemewa kama mito ambayo hukauka. "Njia ya wasafiri hubadili njia kwa ajili ya kutafuta maji"

Misafara

Kifungu hiki kinaweza pia kutafsiriwa kama "njia za misafara" au "njia za wasafiri" au "wasafiri."

huzurura jangwani na kisha huangamia

"hawakwenda popote na kisha hufariki"

Tema

Hili ni jina la mahali. Watu wa mahali pale walitumia misafara kufanya biashara ya vitu na watu kutoka nchi zingine.

wakati majeshi ya Sheba huitarajia

"wakati wasafiri kutoka Sheba waliwatumainia"

Sheba

Hili ni jina la mahali. Watu wa mahala pale walitumia misafara kufanya biashara ya vitu na watu kutoka nchi zingine.

waliwatarajia

"walitumaini kwaajili yao" au " waliweka matumaini yao kwao

Wamevunjika moyo kwa sababu walitumaini kupata maji

"Walichanganyikiwa kwasababu waliamini kwamba wangeweza kupata maji"

lakini walidanganywa

"lakini walipoteza matumaini" au "lakini hawakuridhika"

Job 6:21

Habari za Jumla:

Katika mistari hii, Ayubu anatoa maswali manne kuwakaripia rafiki zake na kusisitiza kwamba yeye hakuomba msaada kutoka kwa yeyote kati yao.

Kwa sasa

Ayubu anatumia kifungu hiki kuanza sehemu kuu ya kile anachosema.

ninyi rafiki si kitu kwangu

"hamtendi kama rafiki zangu"

nanyi mwaogopa

"na ninyi mnaogopa kwamba Mungu anaweza kuwafanyia mambo hayahaya." Hapa inaweka bayana zaidi habari ya kutisha kwamba rafiki zake wanaogopa kuadhibiwa na Mungu.

Je nilisema kwenu, 'Nipeni kitu furani?'

"Sijamuomba yeyote kati yenu kitu chochote."

nitoleeni zawadi katika mali zenu?

"Mimi sijawaomba mnipe pesa." au "Mimi sijawaomba kutoa bibi harusi kwaajili yangu kutoka katika mali zenu."

Niokoeni toka mkononi mwa mtesi wangu?

"Mkono wa mtesi wangu" ni mfano ambao unasimama badala ya nguvu ya mtu fulani ambaye anashindana kwa nguvu sana na Ayubu. "Mimi sijawahi kumwomba mmoja kati yenu kuniokoa kutoka kwa adui zangu"

Niokoeni toka mkononi mwa mtesi wangu?

"Mkono wa mtesi wangu" ni mfano ambao unasimama badala ya nguvu za watu ambao wanamtendea Ayubu vibaya. 'Mimi sijawaomba kuniokoa kutoka kwa wale ambao wananitendea vibaya."

Niokoe

"nisaidie"

Job 6:24

Nifundishe

Kitenzi "kufundisha" ipo katika sehemu ya nafsi ya pili wingi.

nami nitaishika amani yangu

" na mimi nitakuwa kimya"

nifanye nifahamu

"wewe umenifanya mimi nielewe." Kitenzi kipo katika sehemu ya nafsi ya pili wingi.

Jinsi gani maneno ya kweli yanavyo umiza

ULB na UDB zina maana zinazopingana kwa kifungu hiki. Hii ni kwasababu maana mbili zinazofaa kwa Kiebrania ni 1) Maneno ya kweli yanaumiza kuyasikia au 2) Maneno ya mtu mkweli hayaumizi kuyasikia.

Lakini hoja zenu, jee hasa zimenionya nini mimi?

Ayubu anatumia swali hili kuwa karipia rafiki zake na kusisitiza kwamba kile wanachosema hakimhusu. "Sababu zenu hazinihusu japokuwa mmenikosoa bila huruma."

hoja zenu

"Sababu zenu" au "madai yenu." "-ako, - enu" ipo katika sehemu ya nafsi ya pili wingi.

Job 6:26

Je mnapanga kuyapuuza maneno yangu, mnayachukulia maneno ya mtu mwenye kukata tamaa sawa na upepo?

Ayubu anatumia swali hili kuwakemea rafiki zake. "Mmeyapuuza maneno yangu, na kuyachukulia maneno yangu kama si kitu."

Je mna

"wewe, ninyi" ipo katika sehemu ya nafsi ya pili wingi.

mnayachukulia maneno ya mtu mwenye kukata tamaa sawa na upepo

Ayubu analinganisha maneno ya kukata tamaa ya mtu asiye na tumaini kwaajili ya msaada na upepo usio na kitu; yote hayana manufaa.

mna piga kura kwa ajili ya yatima

"hata mna cheza kamari kumpata yatima"

mna piga kura ... kupatana bei juu ya rafiki yenu

Hapa "wewe, ninyi" na "-ako, -enu" yapo katika sehemu ya nafsi ya pili wingi.

na kupatana bei juu ya rafiki yenu kama bidhaa.

"na kuchimba shimo kwaajili ya rafiki yenu"

Job 6:28

Sasa

Neno hili limetumiwa na Ayubu kuleta habari mpya.

tafadhari tazama

Kitenzi "kutazama" lipo katika sehemu ya nafsi ya pili wingi.

usoni penu

"-ako, -enu" lipo katika sehemu ya nafsi ya pili wingi.

punguzeni ukali, nawasihi

"Tafadhari kuwa na huruma nami" au "Tafadhari geuka"

ukali kidogo

Kitenzi hiki kipo katika sehemu ya nafsi ya pili wingi.

lisiwepo neno la uonevu na nyinyi

"nitendeeni kwa haki"

Hasa, punguzeni ukali, sababu zangu ni za haki

"Badilisheni namna mnavyonitendea mimi tena; Mimi niko sawa katika hili" au " Badilisheni namna mnavyonitendea; Mimi bado niko sawa katika hili"

kali kidogo

Kitenzi hiki kipo katika sehemu ya nafsi ya pili wingi.

Je mna uovu ulimini mwangu?

"Je nimesema mabo maovu?" Ayubu anatumia hili swali kuwakemea rafiki zake na kusisitiza kwamba yeye siyo mbaya. "Mimi sisemi mambo maovu."

Je mna uovu ulimini mwangu?

Kiuhalisia ulimi hauwezi kuwa na uovu, kwa hiyo ni mfano uliotumika kuelezea kauli mbaya.

Je kinywa changu hakiwezi kungundua madhara?

Ayubu anatumia swali hili kuwa kemea rafiki zake na kusisitiza kwamba yeye anaweza kuwaambia tofauti kati ya wema na ubaya. "Mimi naweza kuwaambia tofauti kati ya uzuri na ubaya."

Job 7

Job 7:1

Habari za Jumla:

Mwandishi anaendelea kutumia ulinganishaji katika kila mistari hii, kuwasilisha wazo moja akitumia taarifa mbili tofauti kusisitiza kwamba mateso ya mtu binafsi ni sehemu ya mateso ya watu wote ambayo watu wote huyapitia.

Je mtu hana kazi ngumu juu ya nchi?

Ayubu analeta swali hili kusisitiza ufahamu wake kwamba watu wote huyapitia mateso. "Je si kila mtu ana kazi ngumu katika nchi?" au "Kila mmoja ana kazi ngumu katika nchi"

Je siku zake si kama siku za mwajiriwa?

Ayubu anatoa swali hili kuunga mkono ufahamu wake kwamba watu wote hupambana katika maisha. "Na siku zake ni kama siku za mwajiriwa."

Kama mtumwa ... kama mwajiriwa

Ayubu anajilinganisha mwenyewe (mstari 3) na wale ambao hufanya kazi kwa bidii hawana msaada (mstari 2).

kivuli cha jioni

"giza"

mwajiriwa

Huyu ni mtu ambaye hufanya kazi kwa siku kwa muda na hulipwa kutwa ya kila siku. "kibaruwa"

hivyo nami nimeumbwa kuvumilia miezi ya taabu; Nami nimepewa taabu - zimeujaza usiku

kuujaza usiku- "kwa hiyo mimi nimevumilia miezi ya mateso na taabu-zimeujaza usiku"

miezi ya taabu

"miezi ya msiba" au "miezi ya kufirisika"

Job 7:4

Lini nitatoka kitandani na lini usiku utatoweka?

Ayubu analeta swali hili kusisitiza mateso yake makali sana wakati wa masaa ya kulala. "Natamani ningeweza kuamka, lakini usiku unaendelea."

Nimejawa na kujitupa huku na huko

Hii inaonyesha kwamba Ayubu alikuwa anahamahama kitandani usiku kucha bila kupumzika. "Mimi nimechoka kujisukasuka na kujigeuza bila kutulia."

madonda yenye vumbi

uvimbe mchafu

Job 7:6

Habari ya Jumla:

Mwandishi anaendelea kutumia ulinganishaji katika mistari hii, kuwasilisha wazo moja akitumia taarifa mbili tofauti kusisitiza hisia za Ayubu juu ya ufupi wa maisha.

Siku zangu zinakimbia kuliko chombo cha kufumia

"Maisha yangu yanapita haraka sana"

mfumaji

mtu ambaye hutengeneza nguo kwa kupishanisha uzi au kitani

chombo cha kufumia

ni kipande ambacho kinatembea mbele na nyuma haraka sana katika mashine au chombo kwa ajili ya kutengeneza nguo

zinapita bila tumaini

"zinafika mwisho bila matumaini kabisa"

Mungu, anakumbuka

Neno "Mungu" liliongezwa katika kifungu hiki kwa sababu watu ambao watasikia "kumbuka" waliweza kuelewa kwamba Mungu ameandikiwa.

maisha yangu ni pumzi tu

Katika msemo huu, Ayubu analinganisha ufupi wa maisha yake na upungufu wa pumzi. "Maisha yangu ni mafupi kama kupumua mara moja"

jicho langu halitaona mema tena

"Sitapata tena furaha"

Job 7:8

Habari za Jumla:

Mwandishi anaendelea kutumia ulinganishaji katika kila mtistari hii, kuwasilisha wazo moja akitumia taarifa mbili tofauti kusisitiza fikira za Ayubu kwamba, baada ya kufa, si Mungu wala watu yeye alifahamu wataonana naye tena.

Macho ya Mungu yatanitazama, lakini sitakuwako

Neno "Mungu" liliongezwa katika kifungu hiki kwasababu muktadha unaonyesha kwamba Ayubu anaongea na Mungu. "Macho ambayo yananiona mimi hayataniona tena."

Macho ya Mungu yatanitazama, lakini sitakuwako

"Macho yako yatakuwa juu yangu, lakini mimi sitakuwako."

kama vile wingu liishavyo na kutoweka, hivyo wale waendao sheoli hawatarudi tena kabisa

Ayubu anaelezea kifo katika hali ya mawingu yanavyotoweka. "Kama mawingu yatowekavyo, hivyo yeye ambaye anakufa hutoweka" au "Mara wewe uwapo kaburini, hutaweza kuinuka."

kama vile wingu liishavyo

"Kama wingu linavyotoweka"

Job 7:11

Nitasema juu ya maumivu makubwa ya roho yangu; Nitanung'unika juu ya uchungu wa nafsi yangu

Ayubu anawasilisha wazo moja akitumia taarifa mbili tofauti kuelezea sababu za yeye kutokukaa kimya.

sitakizuia kinywa changu

"Mimi sitaacha kuongea"

maumivu makubwa ya roho yangu

"mateso ya moyo wangu" au "maumivu makali ya mateso yangu"

uchungu wa nafsi yangu

"uchungu wa moyo wangu"

Je mimi ni bahari au kiumbe cha kutisha baharini hata ukaweka mlinzi juu yangu?

Ayubu anatoa swali hili kuelezea hasira yake kwa Mungu. Kwa kujilinganisha yeye mwenyewe na bahari au kiumbe cha kutisha baharini, Ayubu anamaanisha kwamba Mungu anamchukulia yeye kama kiumbe cha kutisha. 'Mimi siyo bahari au kiumbe cha baharini ambacho huitaji mlinzi wa kukilinda."

Job 7:13

Habari za Jumla:

Mwandishi anaendelea kutumia ulinganishaji katika mistari miwili ya kwanza, kuwasilisha wazo moja akitumia taarifa mbili tofauti kuelezea maumivu makali sana ya Ayubu.

kitanda changu kitanifariji, na malazi yangu yatatuliza manung'uniko yangu

Hapa "kitanda" na "malazi" ni mifano wa "kulala." Kwa kulala chini, Ayubu alitarajia faraja. Mfano pia una sifa za kibinadamu; wana uwezo wa kumriwadha na kumfariji mtu.

wewe unanitisha mimi

"wewe" inamaanisha Mungu ambaye Ayubu anamlalamikia.

kunyonga

kuua mtu kwa kumkaba koo lake na kuzuia asipumue.

hii mifupa yangu

Hapa Ayubu anatumia neno "mifupa" kumaanisha mwili wake. "Huu mwili wangu"

Job 7:16

Habari unganishi:

Mwandishi anaendelea kutumia ulinganishaji katika mistari hii, kuwasilisha wazo moja akitumia taarifa mbili tofauti kusisitiza matokeo ya mateso ya Ayubu juu ya hisia zake kuwa mwenye thamani.

Ninayachukia kabisa maisha yangu

"Mimi naya-dharau maisha yangu"

siku zote kuwa hai

"kuishi milele"

siku zangu hazifai

"siku zangu hazina maana" au "siku zangu hazina thamani"

hata ukatia bidii kwake

"kwamba wewe utamwangalia yeye"

utaweka akili yako kwake

"kwamba wewe utayaelekeza bidii zako kwake"

na kumwangalia

"kwamba wewe utamwangalia vizuri yeye"

Job 7:19

Je itachukuwa muda gani kabla hujaacha kuniangalia, wala kunisumbua muda wa kutosha kwaajili ya kumeza mate yangu?

Hapa Ayubu anawasilisha wazo moja akitumia maswali mawili ya kejeri kusisitiza matamanio yake kwamba Mungu angeliacha kumwangalia yeye. "Usinitazame! Niache peke yangu kiasi cha kumeza mate yangu mwenyewe!"

Hata kama nimefanya dhambi, itakusaidia nini, wewe ulindaye wanadamu?

Ayubu analeta swali hili kumkaripia Mungu. "Hata kama nimefanya dhambi, kwamba haitakusaidia kitu wewe, ambaye uwalinda watu."

Kwa nini umenifanya shabaha yako, ... kwako?

"Kwanini umenifanya mimi shabaha kwa ajili yako mwenyewe?"

Job 7:21

Kwa nini hunisamehi makosa yangu na kuniondolea uovu wangu?

Hapa Ayubu analeta vishazi viwili tofauti ndani ya swali la kejeri kusisitiza matamanio yake kwamba Mungu atazisamehe dhambi zake. Yeye analeta swali hii kumkaripia Mungu kwa kumfanya ateseke. "Samehe makosa yangu na uniondolee uovu wangu."

Kwa nini wewe husamehi makosa yangu

"Kwa nini husamehi makosa yangu?"

niondolea

"ondoa"

sasa nitalala mavumbini

Kifungu "lala chini katika mavumbi" ni upole au njia ya upole ya kusema "kufa." "sasa mimi nitakufa"

Job 8

Job 8:1

Habari ya Jumla:

Katika kila mstari wa habari yake, Bildadi anawasilisha wazo moja akitumia taarifa mbili tofauti, moja kumkemea Ayubu na tena kumtetea Mungu.

Kisha Bildadi huyo Mshuhi akajibu

"Bildadi" ni jina la mtu ambaye mmoja wa kabila la Washuhi.

Kwa muda gani maneno ya kinywa chako yatakuwa kama upepo wenye nguvu?

Bildadi analeta swali hili kumkaripia Ayubu kwa malalamiko yake kwa Mungu. Katika msemo huu, yote maneno ya Ayubu na upepo ni matupu na dhaifu. "Maneno ya mdomo wako ni upepo wenye nguvu."

Je Mungu hupotosha hukumu? Je Mwenyezi hupotosha haki?

Hapa mwandishi anatumia maswali mawili ya kejeri, ambayo Bildadi anayatumia kukaripia Ayubu. "Mungu hatendi yasiyo haki; Mwenyezi hashindwi kufanya mema."

Job 8:4

kwa kuwa amewatia mkononi kwa makosa yao

" ni kwasababu Mungu ameruhusu uwezo wa dhambi zao kuwaongoza wao" au "amewaadhibu kulingana na matokeo ya dhambi zao."

Lakini wewe unaonaje ukimtafuta Mungu kwa bidii na kufikisha haja yako kwa huyo Mwenyezi

Vifungu vyote hivi vinamtaja Ayubu akimwomba Mungu msaada, au akijitetea kwa Mungu kwa ajili ya msamaha.

ukimtafuta Mungu kwa bidii

"kwa bidii mwombe Mungu kwa ajili ya msaada"

Job 8:6

Ukiwa wewe ni msafi na mkamilifu

"Kama tu wewe ni msafi na mmwenye haki" au " Kama moyo na matendo yako ni mema"

Japokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, hata hivyo hali yako ya mwisho itaongezeka sana

"Hata kama wewe hukuwahi kuwa mwenye heri kabla, wakati wa mwisho wa maisha yako utakuwa tajiri sana."

Job 8:8

Habari ya Jumla:

Mwandishi anaendelea kutumia ulinganishaji katika kila mistari hii, kuwasilisha wazo moja akitumia taarifa mbili tofauti kusisitiza uwezo wa watu kujifunza kutoka kwa wazazi, waliopewa ufupi wa maisha na utayari wa wazazi kuwapa mafundisho.

utie bidii katika hayo mababu zetu waliyojifunza

"Jifunze kwa makini yale waliyoyangundua wazazi wetu" au "zingatia yale ambayo mababu zetu waliyojifunza"

siku zetu duniani ni kivuli

Katika hii tashbiha, maisha yanalinganishwa na giza; yote yanapita kwa haraka.

Je hawatakufunza wao na kukuambia? Je hawatatamka maneno yatokayo mioyoni mwao?

Bildadi anatoa maswali haya kumkaripia Ayubu. "Watakufundisha na kukuambia wewe, na kutokana na uelewa wao unaleta maneno ya kutia moyo."

Job 8:11

Je hayo mafunjo yaota pasipo matope? Je mafunjo yaota pasipo maji?

Bidadi anatoa maswali ya kejeri kusisitiza hoja yake aliyoitoa katika 8:8: Watu wanahitaji mafundisho ya wazazi wao. "Mti wa mafunjo hayawezi kumea mbali na bwawa. Mafunjo hayawezi kumea bila maji."

nyauka

"kausha"

Job 8:13

Habari ya Jumla:

Mistari hii inaendeleza habari ya Bildadi. Katika mstari wa 14 - 15, mwandishi anatumia ulinganishaji, kuwasilisha wazo moja kwa kutumia taarifa mbili tofauti kusisitiza uharibifu wa wale ambao hawajayajenga maisha yao juu ya mafundisho ya wazazi wao.

Hivyo pia ni njia ya wote wamsahauo Mungu

"Kutembea kwenye njia" ni usemi wa kawaida ambao unahusu maisha ya mtu na uelekeo wake. Mara nyingi hii inahusiana na watu kama wanafuata njia ya Mungu au njia zao wenyewe.

matumaini yake ni dhaifu kama utando wa buibui

Hapa Bildadi analinganisha maisha ya waovu na utando wa buibui; nguvu kidogo itaharibu vyote.

atashikamana nayo

"yeye atajaribu kukisaidia hicho"

Job 8:16

Habari za Jumla:

Katika mstari wa 16 - 17, mwandishi anaendelea kutumia ulinganishaji, kuwasilisha wazo moja akitumia taarifa mbili tofauti kueleza ugumu, mfuko wa muda wa kusaidia wa waovu.

Yeye huwa mti mbichi chini ya jua, na machipukizi yake huenea katika bustani yake yote

Hapa Bildadi analinganisha waovu na mti ambao husitawi wakati wa mchana; mwanzoni vyote huonekana hai, mbichi, na bora.

Mizizi yake hujifunga funga kwenye rundo la mawe

Mizizi ya watu waovu hushikamana si katika udongo wenye rutuba lakini kwa mawe. ardhi ya mawe haisaidii mimea kumea. Mizizi ya mtu huyu itakufa mapema. "Mizizi yake hushika kwenye ardhi ya mawe."

huangalia mahali pazuri katikati ya mawe

Neno "wao" inahusu mizizi ya watu waovu. "hutafuta ardhi yenye rutuba miongoni mwa mawe" au "hutafuta udongo wenye rutuba miongoni mwa mawe"

Lakini mtu huyu aking'olewa mahali pake, kisha mahali pale patamkana, na kusema, 'mimi sikukuona

Watu waovu wanalinganishwa na mmea ambao, wakati ukiondolewa kutoka kwenye msingi wa mawe, hautambuliki mahali pote kwasababu hauwezi kustawi katika sehemu yoyote yenye rutuba. "kama hautaondolewa kutoka sehemu yake, utamkana yeye nakusema, 'Mimi sijawahi kukuona wewe."

mahali pale patamkana, na kusema

Uwezo wa mwanadamu kukana na kusema imetumiwa kwa ardhi ya mawe.

mahali pake

"ardhi ya mawe"

Job 8:19

furaha

zawadi, ni matokeo ya tabia ya uovu ya mtu ambayo Bildadi kwa dharau anaitamka kama 'furaha.'

tabia

"matendo" au "namna ya maisha"

mimea mingine itachipuka toka katika udongo ule ule mahali pake

Hapa mwandishi anaendelea na sitiari kutoka 8:16.Watu waovu wanalinganishwa na mimea ambayo huchukua sehemu ya kwanza ya ule ambao humea miongoni mwa mawe. "Wakati mtu muovu mmoja akifa, mwingine atachukua nafasi yake" au "kutoka kwenye udongo, mwingine utamea."

chupuka

"mea"

udongo ule ule

"ardhi ya mawe"

mahali pake

"katika sehemu ya mtu muovu"

wala hatawathibitisha watendao uovu.

"Mkono" ni mfano wa mwili mzima wa mtu. "hatawasaidia watenda maovu" au " hatawatia nguvu watenda mabaya"

Job 8:21

Yeye atakijaza kinywa chako na kicheko, midomo yako na shangwe

Bildadi anaendelea kusema na Ayubu. Neno "yeye" linahusu Mungu, na "-ako, -enu" linahusu Ayubu. Mwandishi anawasilisha wazo moja akitumia taarifa mbili tofauti kuwasilisha furaha ambayo Ayubu atapitia. "Mungu atakupa furaha tena."

midomo yako na shangwe

Maana kamili ya kifungu hiki inaweza kuwafahamika kutokana na mwanzo wa sentensi. "Mungu atakijaza kinywa chako na na kelele za furaha."

Wale ambao wanakuchukia wewe watavishwa aibu; nayo hema yake mwovu haitakuwepo tena

"Waovu watajawa na aibu; wabaya watakoma kuishi."

haitakuwepo tena

"hautadumu" au "utafika mwisho"

Job 9

Job 9:1

"kweli najua kwamba ndivyo hivyo.

"najua kwamba kile unachosema ni kweli"

ndivyo hivyo

Hapa neno "hii" linahusu kile alichosema Bildadi.

kwa namna gani mtu anakuwa na haki kwa Mungu?

"kwa namna gani mtu yeyote atakuwa hana kosa mbele za Mungu?"

hoji

"shindana"

hatamjibu yeye mara moja katika elfu zaidi

"Mara moja katika elfu zaidi" ni usemi unaomaanisha "hata kidogo." Maana zinazofaa ni 1) "hawezi kutoa jibu lolote kwa Mungu" au 2) "Mungu atamjibu yeye hata kidogo"

elfu zaidi

"mara 1,000"

Job 9:4

hekima moyoni

Hapa moyo unawakilisha utu wa ndani au fikira. "ana hekima katika maamuzi yake"

mwenye uwezo mwingi

Jina la kuwazika "nguvu" inaweza kuelezewa kama kisifa "imara." "mwenye nguvu kwa jinsi alivyo imara"

ni nani daima aliyejifanya mwenyewe kuwa mgumu dhidi yake na akafanikiwa?

Hili ni swali la kejeri ambalo linahitaji jibu la "hakuna hata mmoja." Linaweza kupangiliwa kama maelezo. "Hapa mmoja aliyewahi mwenyewe kujifanya mgumu dhidi yake na akafanikiwa."

aliyejifanya mwenyewe kuwa mgumu dhidi yake

Kujifanya mgumu inamaanisha kuwa mkaidi. "kumbishia yeye" au "kumpinga yeye"

ambaye huiondoa milima

"Mungu huhamisha milima"

katika hasira zake

"Hasira" ni jina la kufikirika tu linaweza kuelezewa kama "mwenye hasira" katika kivumishi cha sifa. "kwasababu yeye ni mwenye hasira"

ambaye huitikisa nchi

"Mungu hutikisa nchi"

mihimili yake hutikisika.

"hufanya misingi ya nyumba itikisike"

Job 9:7

ambaye huzihifadhi nyota

"ambaye huzuia nyota zisionekane"

ambaye peke yake ni mwenye kupanua mbingu

Mungu anaongelewa kama aliyeumba mbingu bila msaada wowote, kana kwamba mbingu ilikuwa mfumo kwamba yeye aliueneza.

kuyatuliza mawimbi ya bahari

Mungu anazungumziwa kama mtuliza bahari kana kwamba kwa miguu yake. "hukanyaga miguu yake juu ya mawimbi ya bahari" au " hutuliza mawimbi ya bahari"

Dubu, Orioni, kilima

Haya yanahusu kundi la nyota, ambalo ni kundi la nyota ambalo huonekana kama zimetengeza umbo fulani angani.

Orioni

ni maarufu kwa uwindaji katika elimu ya visasili ya kigiriki

Kilima

nyota nyingi zenye kung'aa ambazo huonekana kama zipo karibu karibu angani.

kundinyota

kundi la nyota ambalo huonekana kama limetengeneza umbo fulani angani

Job 9:10

Habari za Jumla:

Mwandishi anatumia ulinganishaji katika kila mistari hii, kuwasilisha wazo moja akitumia taarifa mbili kusisitiza kwamba Mungu ni mkuu, asiyeonekana, na mwenye mamlaka.

mambo yasiyofahamika

"mambo yasiyochunguzika" au "mambo yasiyoeleweka"

yasiyohesabika

"ambayo hayahesabiki"

Tazama

"Tazama" au "kuwa makini"

hupita kwenda mbele

"yeye hupita" au "yeye huendelea mbele"

Kama akichukua kitu chochote, nani tamzuia? Nani awezaye kumuuliza, 'unafanya nini?'

Haya ni maswali ya kejeri ambayo hutarajia jibu la "Hata mmoja." Yanaweza kupangiliwa kama maelezo. "Kama akichukuwa kitu chochote mbali, hakuna wakumzuia. Hakuna wa kumuuliza, 'unafanya nini?""

Kama akichukua kitu chochote

"Kama yeye akichukua mbali kitu fulani" au "Kama akihitaji kunyakua mbali kitu chochote"

Job 9:13

wamsaidiao Rahabu kuinama chini yake

Hapa "kuinama mbele zake" inaashiria utii au ushindwaji. "yeye huangamiza wasaidizi wa Rahabu"

Rahabu

Neno hili "Rahabu" hapa linamaanisha dubwana la baharini.

Je ni upungufu kiasi gani mimi nitamjibu, je nichague maneno kuhojiana naye?

Ayubu anatoa maswali mawili yanayofanana kusisitiza kukataa kwake kumkabili Mungu. Yanaweza kupangiliwa kama maelezo. "Hivyo Bila shaka mimi nisingeweza kumjibu au kuchagua maneno ya kuhojiana na yeye."

Job 9:16

kwa kuwa yeye anidhoofishaye kwa dhoruba

Ayubu analinganisha mateso yake kutoka Kwa Mungu na athari za dhoruba. "Yeye hunijeruhi mimi kana kwamba kwa dhoruba."

dhoruba

lenye nguvu sana au tufani lenye nguvu sana

zidisha majeraha yangu

"hunipatia mimi majeraha mengi" au "hunijeruhi mimi tena na tena"

pasipo sababu

Hata kama sijaweza kumpa sababu ya kufanya hivyo" au "hata kama sina kosa"

kamata pumzi yangu

Hii ni lugha ambayo humaanisha "pumua" au "vuta pumzi"

yeye hunijaza uchungu

Mstari huu ni mfano wa Mungu kuyajaza maisha ya Ayubu na mambo ambayo humpa yeye uchungu. Jina la kufikirika "uchungu" linaweza kuelezewa kama kivumishi "-chungu." "yeye hunijaza mimi na mambo machungu"

Job 9:19

Kama ni habari ya nguvu

"Kama kuna mabishano ya nguvu"

tazama

"tazama" au "kuwa makini na kile nataka kukuambia"

yeye ni mwenye nguvu

"yeye ni hodari sana"

nani atakaye mhukumu?

Swali hili linatarajia jibu la "Hata mmoja" kutengeneza hoja kwamba hakuna hat mmoja awezaye kumfikisha Mungu mahakamani. Hili linaweza kupangiliwa kama kama maelezo. "hata mmoja anaweza kumuita yeye kortini."

Ingawa ni mwenye haki

Hapa "mimi nipo katika haki" inamaanisha mimi ni mmoja ambaye nimefanya mambo yaliyo haki. "Ijapokuwa mimi nimefanya mambo ya haki" au "Hata hivyo mimi sina kosa"

Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu; na ingawa ni mtakatifu, maneno yangu yatashuhudia kuwa ni mwenye kosa.

mstari huu unaelezea wazo lile lile mara mbili kwa ajili ya kusisitiza.

kinywa changu mwenyewe kitanihukumu

Hapa "kinywa" mfano wa maneno ya Ayubu. "maneno yangu mwenyewe yatanishitaki" au "kile ninachosema kitanihukumu"

mtakatifu

"bila kosa"

maneno yangu yatashuhudia kuwa ni mwenye kosa

Hapa "maneno yangu" yameongelewa kana kwamba yanaweza kutenda jambo. "Mungu atatumia kile ninachosema kuthibitisha mimi ni mwenye kosa"

mwenye makosa

Neno hili hapa linamaanisha "kugeuzwa" au "mdanganyifu."

Job 9:21

Mimi ni mtakatifu

"Mimi ni kamili"

kuhusu mimi mwenyewe

"nini kinanitokea"

Haileti tofauti

"yote ni sawa" au "haina shida"

huangamiza watu wasio na makosa na waovu pia

"yeye huwafikisha kila mmoja mwisho, kama ni wasio na kosa au waovu"

Kama hilo pigo liliua ghafla

"Kama baa linaweza kuua watu ghafra"

mateso ya watu wasio na makosa

Jina la kufikirika "wasio na makosa" linaweza kutafasiriwa kama kitenzi "tesa." "wakati watu wasio na makosa wakiteswa"

Dunia imetiwa

Hii inaweza kusemwa katika hali halisi. "Mungu anatoa nchi"

Dunia

Hapa "nchi" imetumika kuwakilisha watu waishio juu ya nchi. "Watu wa ulimwengu ni"

mkononi mwa

Hapa "mkono" ni mfano wa "udhibiti." "chini ya udhibiti wa"

Mungu hufunika nyuso za waamuzi

Usemi huu unamaanisha Mungu huwasimamia waamuzi wa nchi katika kuweza kuona tofauti kati ya wema na uovu. "Mungu huwapofusha waamuzi" au "Mungu husimamia waamuzi katika kutoa hukumu kwa haki"

kama si yeye hufanya, ni nani basi?

"Kama si Mungu ambaye hufanya mambo haya, halafu nani hufanya haya?"

Job 9:25

Siku zangu zinapita haraka kuliko tarishi akimbiae

Ayubu analinganisha namna siku zake zinavyopita upesi na mkimbiaji mwenye kasi. "Siku zangu zinapita kwa haraka"

tarishi akimbiae

"mkimbiaji" au "mtu anayekimbia"

siku zangu zinakimbia mbali

Hii inazielezea siku za maisha ya Ayubu kama zinaweza kukimbia mbali kama mtu.

hazioni mema mahali popote

Hii inazielezea siku za maisha ya Ayubu kama zinaweza kuona kama mtu.

hakuna mema

"hakuna jambo jema"

Zinapita kwa kasi kama mashua zilizoundwa kwa mafunjo

Ayubu analinganisha namna siku zake zinavyopita kwa upesi na mwendo kasi wa mashua. "Zinapita haraka kama mashua zilizotengenezwa kwa mafunjo"

mashua zilizoundwa kwa mafunjo

"mashua iliyotengenezwa kwa mafunjo." Mafunjo ni majani yenye shimo ambayo humea pembezoni mwa kingo za mito.

zinakasi kama tai ashukaye upesi katika mawindo yake

Ayubu analinganisha namna siku zake zinavyopita upesi na ndege mkubwa ashukaye upesi kuelekea kwenye mawindo. "ana kasi kama tai ashukae chini kwa kasi kukamata chakula chake.

shuka chini kwa kasi

"kuharakisha kwenda chini"

Job 9:27

mimi nitasahau kuhusu manung'uniko yangu

Jina la kufikirika "nung'uniko" linaweza kutafasiriwa kama kitenzi "lalamiko." "Mimi nitaacha kulalamika" au "Mimi nitaacha kulalamika dhidi ya Mungu"

manung'uniko yangu

habari zilizo husika zinaweza kuongezwa. "malalamiko yangu dhidi ya Mungu"

nitaacha kuonyesha sura ya huzuni na kuwa na furaha

Sura yenye huzuni ya Ayubu inaongelewa hapa kana kwamba kitu fulani ambacho kinaweza kuondolewa. "Mimi nitaacha kuonekana mwenye huzuni na kutabasamu"

Mimi nitaziogopa huzuni zangu zote

Mstari wa 28 na 29 zinaelezea matokeo kama Ayubu atafanya yale anayosema katika mstari 27. "Tena mimi nitaogopa kwa ajili ya huzuni zangu"

huzuni zangu zote

Jina la kufikirika "huzuni" linaweza kuonyeshwa kama kitenzi. "nini kitanidhuru"

Nitahukumiwa

"Mimi nitashitakiwa na kuadhibiwa." Hili linaweza kusemwa katika sura ya kutenda. "Mungu atanihukumu"

kwa nini, basi, nitaabike bure?

Ayubu anatumia swali hili kusisitiza kwamba yeye hafikirii kama kuna maana yoyote kujaribu kuupata usikivu wa Mungu. Taarifa za kuashiria kuhusu kile Ayubu anajaribu zinaweza kufanywa wazi. "Haina maana kujaribu kuupata usikivu wa Mungu"

Job 9:30

Kama najiosha mwenyewe kwa maji ya theluj

"Kama nimeoga tu, maji safi"

kuitakasa mikono yangu na kuwa safi zaidi

"kuifanya mikono yangu safi sana." Baadhi ya tafsiri zingine za Biblia zinafasiri hiki na maana ya "nimeosha mikono yangu na sabuni kali sana."

nitumbukize shimoni

"nitupe shimoni"

nguo zangu mwenyewe zitanichukia

Nguo za Ayubu zinazungumziwa kana kwamba zina jibu hasi kwa Ayubu baada ya Mungu kumtumbukiza yeye shimoni. "Mimi nitakuwa mchafu sana kwa ajili ya nguo zangu mwenyewe"

Job 9:32

mjibu yeye

Taarifa za kuashiria zinaweza kuongezwa. "nitajibu mashitaka yake dhidi yangu" au "nitajitetea mwenyewe" au "nitahojiana naye hali yangu yakutokuwa na hatia"

tukaribiane katika hukumu

"tuwe pamoja kwenye hukumu." Hapa "mahakama" ni sehemu ambayo watu wanaweza kuja na hakimu ataamua ugomvi. Kuwa pamoja mahakamani" ni mfano wa kupingana kila mmoja kisheria mahakamani."kila mmoja kutetea upande wake mbele ya hakimu."

Hakuna hakimu baina yetu

Hii inamaanisha hakuna hakimu ambaye ni mkuu kuliko Mungu ambaye anaweza kuamua lipi ni jema kati yake na Ayubu.

weka mkono wake juu

Hapa "weka mkono wako juu ya" inamaanisha kuwa na uwezo au mamlaka zaidi. "uwezo wa kuamua" au "kuwa na mamlaka zaidi"

Job 9:34

Habari unganishi:

Mistari hii inaendeleza hoja ya kwanza kwamba hakuna hata mmoja aliye mkuu kuliko Mungu ambaye anaweza kutenda kama hakimu kati ya Mungu na Ayubu.

niondolee fimbo ya Mungu

Hapa "fimbo ya Mungu" ni mfano wa Mungu anamwadhibu au anamrekebisha Ayubu. "acha Mungu kuniadhibu mimi"

awezaye kuzuia kitisho chake kisinitie hofu

Jina la kufikirika "kitisho" inaweza kutafasiriwa kama kitenzi "tisha." "mzuie kunitisha na kuniogofya mimi"

kisha ningesema

"kisha ningeliweza kusema"

kama mambo yalivyo sasa

"kwasababu hivi ndivyo mambo yalivyo sasa"

Job 10

Job 10:1

Nimechoka na maisha yangu

"mimi nimechoka kuishi"

Nitanena wazi manung'uniko yangu

Jina la kufikirika "usemi" na "lalamiko" yanaweza kutafasiriwa kama vitenzi "eleza" na "nung'unika." "Mimi nitaeleza wazi kile ninachonung'unikia" au "Mimi nitahoji wazi"

nitasema kwa uchungu wa roho yangu

Namna gani Ayubu anavyojisikia inalinganishwa na ladha chungu. Jina la kufikirika "chungu sana" inaweza kutafasiriwa kama kielezi "chungu." "Utu wangu wa ndani utaongea kwa uchungu" au "Kwa uchungu nitasema sana"

ni vizuri kwako wewe kunionea mimi, kudharau kazi ya mikono yako wakati unafurahia juu ya mipango ya waovu?

Swali hili linahitaji jibu la "hapana" na inaweza kubadilishwa na kuwa habari. "Si vyema kwamba unaweza kunikandamiza mimi, kwamba unaweza kudharau kazi ya mikono yako, wakati ukifurahia juu ya mipango ya waovu."

kazi ya mikono yako

Hapa mikono inawakilisha uwezo wa kuumba wa Mungu. "kile ulicho kiumba"

unafurahia juu ya mipango ya waovu

Hapa usemi "ridhia" ni mfano wa kibali cha Mungu."kubali mipango ya waovu"

Job 10:4

Je wewe una macho ya kimwili? Je wewe unaona kama mtu aonavyo?

Mswali haya mawili yanamaana zinazo karibiana. Maswali haya yatarajia jibu hasi kusisitiza kwamba Mungu haoni au kuelewa mambo kama vile mtu aelewavyo. Yanaweza kuelezewa kama habari. "Wewe huna macho ya mwili, na hautazami kama mtu atazamavyo."

Je siku zako ni kama siku za wanadamu au miaka yako ni kama miaka ya watu ... na hapana mwingine awezaye kuniokoa mimi na mkono wako?

Swali hili linatarajia jibu hasi kusisitiza kwamba Mungu ni waa milele na siku za mtu ni ndogo. Linaweza elezewa kama habari. "Siku zako si kama siku za mwanadamu na miaka yako si kama miaka ya watu ... na hapana yeyote ambaye ataweza kuniokoa mkoni mwako."

siku zako ni kama siku za wanadamu ... miaka yako ni kama miaka ya watu

Vifungu hivi viwili vina maana zinazokaribiana.

siku zako

"hesabu ya siku zako"

miaka yako

"hesabu ya miaka yako"

ukauliza habari za uovu wangu ...kutafuta dhambi yangu

Vifungu hivi viwili vinamaana zinazo karibiana.

hata ukauliza

"tena ukatafuta"

kutoka mkoni mwako

Hapa "mkono wako" ni mfano nguvu za Mungu. "kutoka nguvuni mwako"

Job 10:8

Mikono yako

Hapa "mikono" ni mfano wa Mungu na ubunifu wake wa kufanya. "Wewe"

Mikono yako imeniumba na kunifinyanga kwa wakati mmoja nawe kunizunguka

Ayubu anatumia sitiari ya mfinyanzi atengenezaye udongo kuelezea namna Mungu alivyo muumba yeye kwa uangalifu mkubwa.

imeniumba na kunifinyanga

"amenipa umbo na kunitengeneza." Maneno "umbwa" na "finyangwa" yana maana inayolandana.

fikiri

"kumbuka"

utanirudisha mavumbini tena

"nirudishe tena mavumbini"

Job 10:10

Habari za Jumla:

Katika mistari hii, Ayubu anatumia lugha ya ushairi kuelezea namna Mungu alivyo muumba yeye katika tumbo la uzazi.

Je wewe hukunimimina kama maziwa na kunigandisha mfano wa jibini?

Hili ni swali ambalo linatarajia jibu halisi. "Wewe ulinimimina kama maziwa na kunigandisha kama jibini." au "Wewe umenitengeneza mimi katika tumbo la uzazi kama maziwa yamiminavyo na kuwa jibini."

Wewe

Hapa "wewe" linahusiana na Mungu.

mimi

Hapa "mimi" linahusiana na Ayubu.

Umenivika ngozi na nyama

Mungu kuweka ngozi na nyama juu ya mwili wa Ayubu inaongelewa kana kwamba Mungu alimvisha nguo yeye. "Wewe umeweka ngozi na nyama juu ya mwili wangu"

niunganisha pamoja

"umenifuma." Mungu anaunganisha mwili wa Ayubu katika tumbo la uzazi inaongelewa kana kwamba Mungu alikuwa anafuma au anashona kipande cha nguo."niunganishe"

misuri

"mikano." Hizi ni sehemu za mwili ambazo huunganisha misuli na mifupa au sehemu zingine za mwili na ziko kama kwamba ni ngumu, utepe mweupu au kamba nyembamba.

Job 10:12

Wewe umenizawadia mimi uhai na ahadi ya upendeleo

Hapa jina la kufikirika "maisha" linamaanisha maisha ya mwili na "ahadi ya upendeleo" inahusiana na Mungu kuwa mwaminifu kwa ahadi zake. Yanaweza kutafsiriwa kama vitenzi. "Wewe umeniruhusu kuishi na kwa uaminifu hunilinda mimi"

usaidizi wako

"utunzaji wako"

umeilinda roho yangu

Hapa "moyo" inahusiana na maisha ya Ayubu. "umenikinga mimi" au "umenichunga kwa uangalifu sana mimi" au "umeniweka mimi salama"

mambo haya uliyaficha moyoni mwako

Hapa "mambo haya" yanahusiana na mambo yaliyoongelewa katika mistari inayofuata.

mambo haya uliyaficha moyoni mwako

Hapa "umeficha moyoni mwako" inamaanisha Mungu ameyaweka siri au umeyaficha. "mambo haya umeyaweka siri"

wewe utaizingatia

"wewe utanilinda mimi"

Job 10:15

Kama mimi ni muovu

"Kama mimi ni muovu" au "Kama mimi nafanya mambo maovu"

ole wangu

"jinsi ngani itakuwa ya kutisha kwangu"

hata kama ni mwenye haki

"hata kama mimi mara zote hufanya mambo vizuri"

inua kichwa changu

Msemo huu unamaanisha kuwa na uhakika or tumaini. "nitazidi kutazama juu" au "kuwa na tumaini" au "kuwa na uhakika kuhusu mimi mwenyewe"

nimejaa aibu

Jina la kufikirika "aibu" linaweza kutafsiriwa kwa kutumia kivumishi "aibika." "Mimi nimejawa na kuaibika"

aibu

"fedheha"

na ninayaangalia mateso yangu

Jina la kufikirika "mateso" linaweza kutafsiriwa kwa kutumia kitenzi "teseka." "na ninaangalia jinsi gani mimi nateseka"

na ninayaangalia

Neno linalokosekana linaweza kuwa kuongezwa. "na mimi ninatazama"

Kama kichwa changu kikijiinua chenyewe

Msemo huu unamaanisha kuwa kujiamini au kujiona. "Kama nitakuwa na kiburi"

waniwinda kama simba

Maana zinazofaa ni 1) Mungu anamwinda Ayubu kama simba awindavyo mawindo yake au 2) Ayubu ni kama simba awindwaye na Mungu.

mara nyingine tena wajionyesha mwenyewe kuwa ni mwenye nguvu kwangu.

Kifungu hiki kinaelezea kejeri jinsi gani ma ajabu ya nguvu za Mungu yaonekanavyo kwa namna yeye anavyotenda dhidi ya Ayubu.

Job 10:17

Wewe unaleta mashahidi wapya dhidi yangu

Taabu za Ayubu kutoka kwa Mungu zinazungumziwa kana kwamba ni watu ambao wanatoa ushahidi dhidi yake.

na kuzidisha hasira zako dhidi yangu

Jina la kufikirika "hasira" linaweza kutafsiriwa kama kivumishi "mwenye hasira." "na mwenye hasira na mimi zaidi na zaidi"

wanishambulia na majeshi mapya.

Mungu kutuma taabu dhidi ya Ayubu kunazungumziwa kana kwamba Mungu mara kwa mara anatuma majeshi mapya dhidi yake.

Job 10:18

ulinitoa kwenye tumbo la uzazi

Hapa kutolewa nje la tumbo la uzazi kunahusiana na kuzaliwa duniani. "kunitoa mimi nje la tumbo la uzazi la mama yangu" au " kunileta mimi duniani"

ningekata roho

Kukata roho kwa mtu kunahusiana na kufa. "fariki"

na ili jicho lolote lisinione

Ayubu anatumia "jicho" hapa akirejea watu wote. Anatamani yeye angelikufa wakati wa kuzaliwa, kabla hajaonekana na yeyote. "kabla mtu yeyote hajaniona mimi" au "kabla ya kuzaliwa kwangu"

kuwepo

"kuishi"

ningelikuwa nimechukuliwa

"Mwili wangu ungelikuwa umechukuliwa"

Job 10:20

Je si siku zangu pekee ni chache?

Hapa "siku zangu" zinahusiana na urefu wa maisha ya Ayubu. Swali hili linataraji jibu halisi, kusisitiza kwamba Ayubu anatazamia tu kuishi siku chache zaidi. Inaweza kutafsiriwa kama taarifa. "Mimi nina siku chache tu za kuishi zilizobaki."au "Maisha yangu hivi karibuni yatafikia mwisho."

nchi

Hapa sehemu ambayo roho za watu waliokufa huenda inazungumziwa kana kwamba ilikuwa nchi. "sehemu"

kwenye nchi ya giza na kivuli cha mauti

Kifungu "kivuli cha mauti" inaongeza wazo la "giza." Vifungu vyote vinaelezea wapi roho za watu waliokufa huenda.

kivuli cha mauti

Fasiri kifungu hiki kama katika 3:4

giza kama usiku wa manane

Giza la sehemu ambapo roho za watu walio kufa huenda inalinganishwa na giza la usiku wa manane.

bila mpangilio

Hiki kifungu cha kukanusha kinaweza kuelezewa katika hali halisi. "wasiwasi mwingi" au "sehemu ambayo wote wamechanganyikiwa"

ambayo nuru yake ni kama usiku wa manane

Mwanga wa sehemu ambayo roho za watu waliokufa huenda inalinganishwa na usiku wa manane. "ambapo hakuna nuru"

Job 11

Job 11:1

Sofari Mnaamathi

Sofari kutoka sehemu ya Naamathi

Huo wingi wa maneno haupaswi kujibiwa?

Sofari anauliza swali kinyume chake kusisitiza kuwa maneno ya Ayubu lazima yakosolewe."Ni lazima tuyajibu maneno haya yote" au "Mtu yeyote angeyajibu mameno haya yote"

Mtu huyu, aliyejaa maneno mengi awe wa kuaminiwa?

Sofari anatumia swali hili kusisitiza kuwa hawapaswi kuamini kile ambacho Ayubu anachosema. "Mtu huyu amejaa maneno mengi , lakini yeye watu hawapaswi kumwamini" au " Maneno yako mengi peke yake hayamaanishi huna hatia."

Kujivuna kwako kunapaswa kuwafanya wengine wabaki wamenyamaza? "Umeyadharau mafundisho yetu.Sasa tutakufanya wewe ujisikie mweye aibu!

Sofari anatumia swali hili kumkemea Ayubu."Kwa sababu wewe umeongea maneno mengi, hii haimaanishi kuwa wengine lazima wabaki wamenyamaza."

Wakati unapoyadhihaki mafundisho yetu, hakuna awaye yote atakayekufanya wewe ujisikie mwenye aibu?

Sofari anatumia swali hili kumkemea Ayubu "

Job 11:4

Imani yangu ni safi,

"Ufahamu wangu ni sahihi"

Mimi sina waa lolote machoni pako.'

Macho yanawakilisha kuona , ni tashbiha ya tathimini juu ya Mungu kwa Ayubu. Maana zaweza kuwa 1) Ayubu anasema kwamba Mungu amemhukumu yeye kama asiye na hatia" au 2) kwamba Ayubu anaamini yeye amekuwa asiye na hatia na kwamba Mungu anapaswa kumhukumu yeye kama mwenye hatia. "Mnapaswa kutambua kwamba mimi sina hatia."

laiti, Mungu huyo angesema na kufungua midomo yake dhidi yako;

Maneno "kufungua midomo yake" ni ishara ambayo inamaanisha zungumza. Sentensi hizi mbili zinamaanisha kitu kilekile zimetumika pamoja kusisitiza shauku ya Sofari kuwa Mungu angezungumza kwa kumuumiza Ayubu.

hivyo angekuonyesha wewe siri za hekima1

Ni nini "siri za hekima". Zinaweza kuelezwa wazi hivi: "kwamba yeye angekuonyesha wewe kuwa wewe unateseka kwa sababu ya dhambi yako"

Mungu anataka kutoka kwako kidogo kuliko uovu wako unavyostahili.

Kutaka kutoka kwa Ayubu inawakilisha kuadhibiwa kwa Ayubu. "Mungu anakuadhibu wewe kidogo kuliko wewe unavyostahili"

Job 11:7

Je, wewe unaweza kumfahamu Mungu kwa kumtafuta yeye? Unaweza kumtambua aliye mkuu kwa ukamilifu?

Haya maswali mawili ya mfano yanauliza kitu kile kile. Mwandishi anatumia mfumo wa maswali kuongeza msisitizo."Wewe huwezi kumfahamu Mungu kwa kumtafuta yeye, na wewe hautaweza kabisa kumfahamu aliye mkuu"

Upeo

Hii inamaanisha kumfahamu Mungu.

uko juu kama mbingu; unaweza kufanya nini wewe ? Ni wenye kina kirefu kuliko kuzimu;

Kutokuweza kumfahamu Mungu kumezungumzwa kuwa kama vile ilikuwa haiwezekani kwenda mbali mahali pa kuzimu. "haifikiwi kama mahali pa juu mbinguni ....haifikiwi zaidi kuliko mahali pa chini pa kuzimu"

unaweza kufanya nini wewe ?

Sofari anatumia swali hili kuonyesha kuwa mtu hawezi kufanya chochote kumfahamu Mungu kabisa."wewe huwezi kufanya chochote" au " wewe huwezi kumfahamu yeye kikamilifu"

waweza kufahamu nini wewe?

Sofari anatumia swali hili kuonyesha kwamba mtu hawezi kumfahamu Mungu kwa ukamilifu."Wewe huwezi kumfahamu Mungu kwa ukamilifu" au wewe huwezi kufahamu yale yote ya kufahamu"

Vipimo vyake

Ukuu wa Mungu, au ukuu wa hekima

ni virefu kuliko nchi, na vipana kuliko bahari.

Ukuu wa Mungu au hekima umezungumzwa kama unaweza kupimwa katika umbali.

Job 11:10

kama yeye.... kumyamazisha mtu yeyote,

"Kama Mungu ...akimfunga mtu yeyote gerezezani"

kama yeye akimwita mtu yeyote hukumuni,

Jina dhahania "hukumu" laweza kutafsiriwa pamoja na tendo "hukumu." "kama Mungu akimwita mtu yeyote kwake hivyo kwamba Mungu angemhukumu yeye"

ni nani anayeweza kumzuia yeye?

Swali hili linasisitiza kuwa hakuna hata mmoja awezaye kumzuia Mungu. "Hakuna awezaye kumzuia yeye!"

hawezi yeye kuukumbuka?

Hii kinasisitiza kuwa Mungu anakumbuka dhambi. "Hakika yeye huikumbuka !

Lakini watu wapumbavu hawana ufahamu;

Jina dhahania "ufahamu" laweza kuelezwa pamoja na kitenzi "fahamu." "Lakini watu wapumbavu hawafahamu"

wataupata wakati punda mwitu atakapozaa mtu.

Kwa kuwa punda mwitu hawezi kuzaa mtu, maneno haya yanamaanisha kwamba watu wapumbavu hawatapata ufahamu. "ni pale tu ikiwa punda mwitu atakapozaa mtu ndipo watu wapumbavu watapata ufahamu" au "haiwezekani kwa mtu mpumbavu kupata ufahamu kama ilivyo kwa punda kuzaa mtu."

Job 11:13

ikiwa umeuelekeza moyo wako kwa haki

Moyo huwakilisha fikra na mitazamo. Kuuelekeza inawakilisha kuusahihisha. "hata kama wewe umeusahihisha mtazamo wako."

na umeunyosha mkono wako karibu na Mungu;

Hiki ni kitendo cha ishara kuwakilisha kumwomba Mungu msaada. "na amefanya kusihi, ameomba kwa Mungu.

ikiwa huo uovu ulikuwa katika mikono yako

Mkono unawakilisha kile ambacho mtu anakifanya. "hata ikiwa wewe umefanya vitu viovu katika wakati uliopita."

lakini hivyo tena unauweka mbali nawe,

Kuiweka dhambi nyuma inawakilisha kuacha kutenda dhambi. "lakini kwamba tena wewe unaacha kufanya dhambi."

haukuruhusu kutokuwa mwenye haki kukaa hemani mwako.

Maisha yasiyo ya haki yanawakilisha watu kufanya mambo yasiyo ya haki. "na wewe hukuwaruhusu watu wa nyumba yako kufanya mambo yasiyo ya haki."

Job 11:15

inua juu uso wako bila ishara ya aibu;

"Inua juu uso wako" inawakilisha mtazamo wa mtu mwenye kujiamini na ujasiri"

ungeyakumbuka hayo tu kama maji ambayo yametiririka mbali.

Sofari analinganisha ukiwa na maji ambayo hutiririka chini na yanapotea. "Wewe ungeyakumbuka, lakini mateso yatatoweka kama maji ambayo yametiririka mbali.

Maisha yako yangekuwa angavu kuliko adhuhuri;

Sofari anarudia wazo lile lile kwa msisitizo.

Maisha yako yangekuwa angavu kuliko adhuhuri

mga'o unawakilisha kuwa mwenye mafanikio na furaha. "Maisha yako yangefanikiwa na furaha kama adhuhuri"

japokuwa kulikuwa na giza,

giza linawakilisha mahangaiko na huzuni."Ingawa kulikuwa ya giza na huzuni"

itakuwa kama asubuhi.

Asubuhi inawakilisha mwanga, ambao unawakilisha mafanikio na furaha. "yatakuwa mafanikio na furaha kama asubuhi"

Job 11:18

Ungekuwa salama...utachukua pumziko lako katika usalama.

Sofari anarudia wazo lilelile kwa msisitizo na anaelezea uwezekano.

utachukua pumziko lako katika usalama

"Chukua pumziko lako" ni nahau kwa "pumziko" maneno" katika pumziko" yanaweza kuelezwa pamoja na neno" salama" ungepumzika salama"

Pia ungelala chini katika pumziko,

Sofari anarudia wazo lilelile kwa msisitizo na anaelezea uwezekano.

ungelala chini katika pumziko

jina dhahania "pumziko" kinaweza kuelezwa pamoja na kitenzi "pumzika" "wewe ungelala chini na kupumzika"

Job 11:20

macho ya watu waovu yatashindwa;

Macho yao yanawakilisha ufahamu wao. "ufahamu wa watu waovu utashindwa" au "watu waovu hawataweza kufahamu"

tumaini lao la pekee litakuwa pumzi yao ya mwisho ya uhai.

Jina dhahania "tumaini" chaweza kuelezwa pamoja na kitenzi "tumaini" pumzi ya mwisho ya uhai inawakilisha kufa. " "Tumaini lao pekee litakuwa pumzi yao ya mwisho" au " watatumaini kufa tu"

Job 12

Job 12:1

Hakuna shaka

"Hakika"

ninyi wanadamu

"ninyi ni watu muhimu mnafahamu kila kitu"

Hakuna shaka ninyi wanadamu; Hekima mtakufa nayo

Ayubu anawadhihaki jinsi gani wanavyotenda na kuonyesha jinsi walivyo wenye kudhihaki. "Hakika ninyi ni watu muhimu kwamba hekima haiwezi kuwepo bila ninyi" au " Ninyi nyote mnatenda kama ninyi ni watu wenye hekima peke yenu, na kwamba wakati mtakapokufa hekima itapotea"

ninyi

Huu ni wingi hapa na katika sentensi mbili zifuatazo.

Ni dhahiri, ni nani asiyefahamu vitu hivyo kama hivi?

Ayubu anatumia swali hili kuelezea ukweli ambao unapaswa kuwa wazi kwa wasikilizaji wake. Sentensi hii inaweza kuelezwa kwa jinsi hii: Ni dhahiri hakuna awaye yote ambaye hafahamu vitu kama hivi" au "kila mtu anafahamu vitu hivi"

Job 12:4

Mimi ni kitu cha kuchekwa na jirani-Mimi, ni mmoja aliyemwita Mungu na ambaye alijibiwa na yeye!

Uhusiano baina ya tungo hizi unaweza kufafanuliwa na maneno " japokuwa" "Mimi ni kitu cha kuchekwa na jirani zangu-ingawa ni mmoja aliye mwita Mungu na yeye alinijibu mimi"

Mimi, ni mwenye haki na mtu asiyekuwa na hatia-Mimi sasa nimekuwa kitu cha kuchekwa.

Uhusiano kati ya tungo hizi "japokuwa" "Japokuwa mimi ni mwenye haki na mtu asiyelaumika, sasa watu ananicheka"

Katika mawazo yake mtu fulani aliye katika kufurahi, kuna kudharau kwa mashaka;

Maneno " mawazo", "rahisi" "dhihaka" "bahati mbaya"yaweza kuelezwa pamoja na tungo zingine. "Mtu anayeishi katika maisha rahisi humchukia mtu anayeteseka"

huleta mambo mabaya zaidi kwa wale ambao miguu yao inateleza.

Kuleta mambo mabaya ina maanisha kuyasababisha kutokea. "kusababisha vitu vibaya zaidi kutokea"

ambao miguu yao inateleza

Mguu kuteleza inamaanisha kuwa katika hatari au mahangaiko"

Hema za wezi hufanikiwa,

Kufanikiwa kwa hema zao kunawakilisha wezi kufanikiwa katika hema zao. "Wevi huishi katika kufanikiwa ndani ya hema zao wenyewe"

mikono yao wenyewe ni miungu wao.

"Mikono yao wenyewe" kiwakilishi cha "nguvu na " na "miungu yao" ni tashbiha kuelezea kiburi chao. "wao wanajivuna sana kwa uwezo wao wenyewe"

Job 12:7

7Lakini sasa waulize... watakuambia wewe.

Tungo hizi nne zote zinaelezea wazo moja kwamba wanyama wa mwituni, ndege, ardhi, na samaki, wanamfahamu Mungu vizuri kuliko rafiki za Ayubu wanavyofanya.

waulize hao wanyama wa mwituni, na watakufundisha wewe;

Kiambishi tashihisi katika sehehemu ya kwanza ya sentensi kinatumika kuonyesha hali ya kutokuwa na uhakika wa jambo kutokea. "Lakini ungewauliza hayawani wangekufundisha wewe"

waulize ndege wa angani, na watakuambia wewe

Tashihisi katika sentensi hii inatumika kuonyesha hali ya kutokuwa na hakika ya jambo kutokea. "kama wewe ungewauliza ndege wa angani, wao wangekuambia wewe"

Au iambie ardhi, na itakufundisha wewe;

Kiambishi tashihisi katika sehemu ya kwanza ya sentensi hii kinatumika kuonyesha hali ya kutokuwa na uhakika wa jambo kutokea "Au kama ungeiambia ardhi ingekufundisha wewe"

samaki wa baharini watakutangazia wewe.

Kiambishi tashihisi "Waulize samaki wa baharini" kimefahamika kutoka katika sentensi zilizotangulia."na kama ungeliwauliza samaki wa baharini, wangekutangazia wewe"

Job 12:9

Ni myama yupi miongoni mwa hawa asiyefahamu kuwa mkono wa Yahwe umetenda haya

Swali hili linasisitiza mantiki ya kwamba wayama wote wanatambua kuwa Yahwe amefanya haya. Ina maanisha , "Kila mnyama anafahamu....haya."

mkono wa Yahwe umetenda haya?

Mkono wa Yahwe unawakilisha nguvu zake. "Yahwe ametenda haya kwa nguvu zake"

Katika mkono wake mna uzima...na pumzi ya wanadamu wote.

Mkono wa Yahwe unawakilisha udhibiti wake au nguvu. Vitu kuwa katika mikono yake inawakilisha uweza wake kuvidhibiti. "ambaye anadhibiti uhai wa kila kiumbe hai na ataoa uhai kwa kila mwanadamu"

pumzi ya wanadamu

"Pumzi" inawakilisha uzima au uwezo wa kuishi

Job 12:11

Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile kaakaa lionjavyo chakula chake?

Ayubu anatumia swali hili kusisitiza kuwa watu husikiliza kile ambacho watu husema na kuhukumu ikiwa ni vizuri au hapana. Sikio na kaakaa ni mfano wa kusikia na kuonja. " Huwa tunasikia kile ambacho watu husema na kukionja kama vile tunavoonja chakula"

Kwa wazee mna hekima;

"Watu wazee wana hekima" kivumishi cha jina "hekima" chaweza kuelezwa pamoja na "ufahamu." Neno "watu" linamaanisha watu wote kwa ujumla. "watu wazee ni wenye hekima"

katika wingi wa siku mna ufahamu.

Tungo "wingi wa siku" ni kuonyesha kuishi kwa muda mrefu.Ufahamu uko katika wingi wa siku kuwakilisha watu kupata ufahamu wakati wanapoishi muda mrefu. Kivumishi cha jina "ufahamu" kinaweza kuelezwa na tungo "ufahamu mwingi" "Watu hupata ufahamu mwingi wakati wanapoishi muda mrefu" au " Watu ambao huishi muda mrefu hufahamu mengi"

Job 12:13

habari za Jumla:

Mstai wa 13 unasema kuwa Mungu ni mwenye hekima na mkuu. Mwisho wa sura hii inaonyesha kuwa hii ni kweli kwa kuzungumza kuhusu mwenye hekima na vitu vikuu ambavyo Mungu hufanya.

Pamoja na Mungu mna hekima na ukuu

Kivumishi cha jina "hekima" na" ukuu" vyaweza kuelezwa na kivumishi "busara" na "ukuu Mungu ni mwenye hekima na "ukuu"

Tazama

Neno hili linamkumbusha Ayubu wakati Ayubu alipohitaji msikilizaji kuwa na mwitikio maalumu.

haiwezekani kujengwa tena;

Sentensi hii yaweza kuelezwa kwa jinsi hii: "Hakuna awezaye kujenga tena"

kama yeye akimtia gerezani mtu yeyote, hakutakuwa tena kufunguliwa

Kama Mungu akimfunga mtu yeyote, hakuna awezaye kumfungua yeye."

kama yeye akiyazuia maji, yanakauka

Maana zaweza kuwa: 1)kuizuia mvua isinye. "kama akiizuia mcvua isinyeshe ardhi hukauka" au 2) kuzuia maji yasitiririke . " "kama yeye akiyazuia maji yasitiririke, ardhi hukauka"

kama akiyaachilia nje yanaitaabisha nchi

Maana zaweza kuwa: 1)kufanya mvua inyeshe) 2"kama akaiifanya mvua kubwa kunyesha, huigharikisha nchi" au" kuyafanya maji yafurike "kama akiyafanya maji mengi kufurika, huigharikisha nchi"

Job 12:16

Pamoja na yeye mna nguvu na hekima;

"Mungu ni mwenye nguvu na hekima"

watu ambao wamedanganywa na mdanganyi wote pamoja wako katika nguvu zake.

Kuwa katika nguvu za Mungu inawakilisha Mungu anatawala juu yao. "Watu ambao wanauamini uongo, na watu ambao huwadanganya wengini wote pamoja wako katika nguvu zake" au " Mungu anatawala juu ya wote wanaouamini uongo na watu ambao huwadanganya wengine"

Yeye huwaongoza washauri mbali bila kuvaa viatu

Kuwaongoza washauri mbali bila kuvaa viatu huwakilisha kuondolea mbali hekima yao na mamlaka yao.

katika huzuni;

Kielezi cha jina "huzuni" kinaweza kuelezwa pamoja na maneno "majonzi" msiba" "na wanajisikia wenye huzuni sana" au na wana majonzi"

huwarudisha hakimu katika upumbavu.

"yeye huwafanya wahukumu kuwa wapumbavu"

Yeye Huondoa minyororo ya mamlaka kutoka kwa wafalme;

Maaana zaweza kuwa: 1) kuwafanya wafalme kutokuwa na mamlaka tena. "Yeye huondoa mamlaka ya wafalme" au 2) huu ni mfano wa kuwaweka watu huru kutoka katika minyororo ambayo wafalme wameiweka juu yao) "yeye huondoa utumwa ambao wafalme wameuweka juu yao."

yeye hufunika viuno vyao kwa nguo.

Nguo hii huenda ambayo mtumwa huvaa. Kuvaa nguo hizi kwa wafalme inawakilisha kuwafanya wafalme kuwa watumwa" au " yeye huwafanya kuwa watumwa"

Job 12:19

Yeye huwaongoza makuhani mbali bila kuvaa viatu

Kuwaongoza makuhani mbali bila kuvaa viatu inawakilisha kuondolea mbali mamlaka yao.

Yeye humwaga aibu

"aibu" inaweza kuelezwa kuwa ni huzuni, au majonzi." na wanajisikia wenye huzuni zana"

kuwapindua watu wakuu.

"huwashinda watu wenye nguvu"

Yeye huondoa hotuba ya wale waliokuwa wameaminiwa

Kuondoa hotuba zao kunawakilisha kuwafanya wao washindwe kuzungumza."Yeye huwafanya wale waliokuwa wameaminiwa kutoweza kuzungumza" au "Yeye huwanyamazisha watu ambao wengine wanawatumainia"

huondoa mbali ufahamu wa wazee

Kuondolea mbali uafahamu wao kunawakilisha kutoweza kufahamu au kufanya maamuzi sahihi. "huwafanya wazee washindwe kufahamu: au " huwafanya wazee wasiweze kufanya maamuzi sahihi"

wazee.

"watu wazee" au" wazee"

Yeye humwaga aibu juu ya binti za wafalme

Kumwaga aibu juu ya binti za wafalme ni kuwasababishia watu kujisikia wenye huzuni juu yao." Yeye huwafanya watu kutowaheshimu sana wale wanaotawala"

hufungua mishipi ya watu wenye nguvu.

Mshipi ni alama ya nguvu.Kufungua mshipi wa mtu menye nguvu huwakilisha kuondolea mbali nguvu zake na kumfanya awe dhaifu"

Job 12:22

Yeye huweka wazi vitu vya kina kutoka katika giza

Kuviweka wazi vitu ikiwa ni kuvifanya vijulikane. " Vitu vya kina kutoka katika giza" huwakilisha siri ambazo watu hawazijui. "Yeye huzifanya siri kujulikana ambazo watu hawazifahamu"

kuvileta nje kumuika vivuli mahali ambapa watu waliokufa wapo

Kuvileta vitu nje inawakilisha kuvifanya vijulikane."hufanya mahali ambapo wafu waliko pajulikane"

huyafanya mataifa kuwa na nguvu

"Yeye hufanya kupanuka kwa nchi ya watu waliojikusanya pamoja kuwa kubwa" au " Yeye hufanya mataifa kuchukua ardhi zaidi"

pia yeye huyaongoza mbali kama wafungwa.

Mungu kuyaongoza mataifa kunawakilisha Mungu kuwafanya adui za mataifa kuwaongoza. Neno "wao" linawakilisha watu wa mataifa hayo. " Yeye pia huwafanya adui zao kuwaongoza wao mbali kama wafungwa"

Job 12:24

Yeye huondoa mbali ufahamu kutoka kwa viongozi wa watu wa nchi

Kuondolea mbali ufahamu wao inawakilisha kuwafanya wao wasiweze kufahamu"Yeye huwafanya viongozi wa watu wa nchi kutoweza kufahamu.

kutangatanga msituni mahali pasipo na njia.

Kutangatanga nyikani mahali pasipo na njia kunawakilisha kuwa katika wakati mgumu na kutokujua nini cha kufanya. "kuwa na hakika ya nini cha kufanya kama mtu anayetangatanga katika nchi ya uharibifu pasipo na njia.

Wao wanapapasa katika giza bila kuwa na mwanga

Kuwa katika giza bila mwanga kunawakilisha kukosa maarifa ."Wao wanahangaika kufanya maamuzi bila kuwa na maarifa kama vile watu wanavyohangaika kutembea katika giza bila mwanga.

yeye huwafanya wao kuweweseka kama mtu mlevi.

Kuweweseka au kutangatanga kama mtu mlevi kunawakilisha kuishi bila matumaini kama mtu mlevi ambaye huweweseka anapotembea.

Job 13

Job 13:1

Sentensi Unganishi:

Sentensi unganishi: Ayubu anaendelea kuzungumza kwa rafiki zake.

Tazama

"Kuwa msikivu" au "Sikiliza" "maneno haya yanakumbusha pale Ayubu anapowataka rafiki zake kusikiliza kwa makini"

jicho langu limeyaona haya yote;

Ayubu anajisema yeye mwenyewe kama macho yake kwa kuwa ni macho yake ambayo yanaona vitu hivi. "Mimi nimeyaona haya yote"

sikio langu limeyasikia na kuyaelewa hayo.

Ayubu anasema yeye mwenyewe kama sikio lake kwa kuwa kwa masikio yake yeye mwenyewe amesikia vitu hivi. "Mimi nimesikia na kuvielewa"

Kile mnachokifahamu, ndicho hicho mimi pia ninachokifahamu;

Kile mnachokifahamu, Mimi pia ninakifahamu" au "Mimi ninafahamu mengi kama vile ninyi"

Job 13:3

Mimi natamani kusemezana na Mungu.

Rafiki za Ayubu wanamhukumu yeye, lakini hawazungumzi ukweli. Ayubu zaidi angehojiana na Mungu kuhusu malalamiko yake .

ninyi mnauficha ukweli kwa uongo;

Kuweka uongo au kuufunika uongo inawakilisha kuupuuza ukweli. "ninyi mnauficha ukweli kwa uongo" au " niniyi mnadanganya na kuupuuza ukweli"

ninyi nyote ni tabibu msiokuwa na thamani

Kuwa tabibu inawakilisha kuwa mtu ambaye huwafariji wengine. Kuwa asiye na thamani ina maanisha kwamba wao hawafahamu jinsi ya kufanya kile wanachopaswa. "Ninyi nyote ni kama tabibu ambao hawajui kuwaponya watu" au " ninyi nyote mnakuja kunifariji mimi, lakini hamtambui jinsi ya kufanya, kama tabibu asiyekuwa na weledi"

shikilieni amani yenu!

Inamaanisha: "nyamazeni "au acheni kuzungumza"

Hilo lingekuwa hekima yenu ninyi.

Walidhani kuwa walikuwa wanasema vitu vya busara lakini Ayubu alikuwa anasema kwamba wanapaswa kuwa wenye busara kama wangeacha kuzungumza. Kielezi cha jina "hekima" Chaweza kuelezwa na neno "busara" "kama niniyi mngefanya hivyo, ninyi mngekuwa wenye busara" au " kama ninyi mngeacha kuzungumza, niniyi mngeonekana wenye busara"

Job 13:6

Sentensi Unganishi:

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa rafiki zake.

Sikiliza kusihi kwa midomo yangu mwenyewe

Hapa neno "midomo" linawakilisha mtu anayezungumza. "sikiliza kile ambacho mimi mwenyewe nikusihi"

Ninyi mtazungumza visivyo haki kwa ajili ya Mungu, na ninyi mtazungumza udanganyifu kwa yeye?

Ayubu anatumia maswali haya mawili kuwakemea rafiki zake kwa kuzungumza visivyo haki. "Ninyi mnafikiri kwamba mnazungumza kwa Mungu, lakini mnazungumza visivyo haki." Ninyi mnazungumza udanganyifu"

mtazungumza udanganyifu

"uongo", sema "uongo"

Ni kweli ninyi mngetetea katika mahakama kama mawakili wa Mungu?

Kuonyesha upole kwa Mugnu kunawakilisha kumsaidia Mungu au kumtetea Mungu dhidi ya malalamiko ya Ayubu. Ayubu anatumia maswali haya mawili kuwakemea rafiki zake kwa kufikiri kwamba wanaweza kumtetea Mungu. " Ninyi mnafikiri kuwa mnaweza kumtetea Mungu. Ninyi mnafikiri mnaweza kutetea kama mawakili wa Mungu katika mahakama"

Job 13:9

Je, kweli ingekuwa vizuri kwenu wakati yeye akiwatafuta ninyi

"Kuwathibitisha ninyi" ni tashbiha inayomaanisha " jitathimini ninyi" Ayubu anatumia swali hili kuwatahadharisha rafiki zake kuwa ikiwa Mungu angewatathimini wao, yeye angesema kwamba matendo yao ni mabaya. "Kama Mungu angewatathimini ninyi, isingekuwa vyema kwenu"

Mngeweza ninyi kumdanganya yeye kama mlivyoweza kuwadanganya watu?

Ayubu anatumia swali hili kuwaonya rafiki zake kuwa Mungu anaujua ukweli kuhusu wao. "Ninyi mngeweza kuwadanganya wanadamu, lakini ninyi hamuwezi kumdanganya Mungu"

mjithibitisha ninyi

"mjisahihisha ninyi"

ikiwa katika siri ninyi mmeonyesha kutokukamilika.

Kuonyesha kutokukamilika inamaanisha kusema tu mambo mazuri ili kwamba hakimu atasema kwamba mtu yule ni mwema. Kufanya hivi kwa siri inamaanisha kujifanya kuzungumza kwa haki, lakini kiukweli kumpendelea mtu mmoja dhidi ya mwingine. "kama ninyi mnaonyesha upendeleo kwa siri kwa mwingine"

Job 13:11

Je, ukuu wake usingewafanya ninyi muogope? Je, utisho wake usingeshuka juu yenu?

Ayubu anatumia swali hili kuwakemea rafiki zake: Sentensi hii yaweza kutafsiriwa hivi: 1) Ayubu anasema kuwa wanapaswa kumhofu Mungu " Ukuu wake unapaswa kuwafanya ninyi muogope, na ukuu wake unapaswa kushuka juu yenu" au 2) Ayubu anasema kwamba wao watamhofu Mungu." Ukuu wake utawafanya ninyi muogope na utisho wake utashuka juu yenu"

Je, utisho wake usingeshuka juu yenu?

Utisho wake kushuka juu ya watu inawakilisha wao kuogopa sana "Ninyi hamtaogopeshwa sana" au " Ninyi hamtaogoa sana?

Hadithi zenu za misemo ya kukariri, ni mithali zimetengenezwa kwa majivu;

Majivu yanawakilisha vitu ambavyo havina thamani na havidumu. "Hadidhi zenu hazina thamani kama majivu" au "Misemo yenu ya kukariri itasahaulika kama majivu yaliyomwagwa mbali"

utetezi wenu ni utetezi uliotengenezwa kwa udongo wa mfinyanzi.

Ayubu anazungumza kile ambacho wanasema kama vile kilikuwa kama ukuta kuzungumza mji uliotengenezwa kwa majivu; Hauwezi kuwalinda watu kwa sababu udongo wa mfinyanzi huvunjika kirahisi."Ninyi mnasema nini katika utetezi kama vile ni upuuzi kama ukuta wa udongo wa mfinyanzi.

utetezi wenu

Hii inamaanisha kwa kile wanachokisema kujitetea wao wenyewe. au 2) kile wanachokisema kumtetea Mungu.

Job 13:13

Shikilieni amani yenu

Hii ni nahau ionayomaanisha "Nyamaza" au Acha kuzungumza"

mniache peke yangu,

Hii ni nahau yenye maana ya "acheni kunivunja moyo mimi au " acheni kunizuia mimi"

acheni yaje yale yanayoweza kuja kwang

Vitu vinakuja juu ya mtu inawakilisha vitu vinavyotokea kwa mtu. Ni kuonyesha kinachoanza na "Acha" maana yake yeye hajali kile kinachoweza kutokea kwake. " Acheni chochote kinachoweza kutokea kwangu kitokee" au " Sijali kile ambacho kinaweza kutokea kwangu"

Nitaichukua nyama yangu mwenywewe katika meno yangu;

"Nyama" kuwakilisha maisha. "Meno" na "mikono" ni kiwakilishi cha udhibiti wake. Tungo hizi mbili pamoja zinasisitia kuwa Ayubu yuko tayari kuhatarisha maisha yake kwa kutetea hoja yake pamoja na Mungu. " Niko tayari kuyahatarisha maisha yangu"

Job 13:16

Hiki kitakuwa sababu ya kutohesabiwa hatia,

Kielezi cha jina "kutohesabia hatia" chaweza kuelezwa pamoja na kitenzi " kutohesabia hatia" "Hii ndiyo sababu Mungu hatanihesabia hatia mimi " au " Hii ni sababu ambayo Mungu atasema kwamba mimi sina hatia"

Mungu, sikiliza kwa makini

Ayubu anaanza kuelekeza hoja yake moja kwa moja kwa Mungu.

sikiliza kwa makini kuzungumza kwangu; ruhusu kutangaza kwangu kuje kwenye masikio yako.

Mistari hii miwili kimsingi inamaanisha kitu kilekile na kinatilia uzito wa ombi la Ayubu kwa Mungu kumsikiliza yeye.

ruhusu kutangaza kwangu kuje kwenye masikio yako.

Kielezi cha jina "tangazo" Chaweza kuelezwa pamoja na kitenzi "tangaza." Masikio yanawakilisha kusikiliza. "sikiliza kutangaza kwangu" au sikia kile ninachotangaza"

Job 13:18

Habari za Jumla:

Ayubu anaendelea kuzungumza na Mungu

Tazama sasa

Huu ni msisitizo wa kile kinachofuata." Sikiliza sasa" au "tafadhali, kipekee, sikiliza."

Nimeuweka utetezi wangu katika mpangilio,

Ameupangilia utetezi wake ni kuamua kile ambacho angesema kujitetea yeye mwenyewe. " Mimi nimefikiria jinsi nitakavyojitetea mwenyewe" au "Mimi nimeamua jinsi nitakavyojieleza mimi mwenyewe"

Ni nani anayeweza kushindana na mimi katika mahakama?

Ayubu anatumia swali hili kueleza imani yake kwamba kwa kuwa yeye yuko sahihi, hakuna awaye yote angeshindana na yeye. "Mimi siamini kuwa mtu yeyote atahojiana na mimi katika mahakama."

Ikiwa mlikuja kufanya hivyo,

"kama mlikuja kushindana dhidi yangu mimi"

ikiwa ninyi

"Ninyi" hapa ina maanisha Mungu mwenyewe.

kama mimi nilithibitishwa kukosea,

"Kama niniyi mngethibitisha mimi kuwa nimekosea"

kuyatoa maisha yangu.

"Kuyatoa maisha ya mtu ni tashbiha inayomaanisha kufa"

Job 13:20

Habari za Jumla:

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa Mungu.

kutoka katika uso wako.

"Uso" unawakilisha mtu. "kutoka kwako wewe"

Ondoa kutoka kwangu mkono wako unaotesa,

Kuondoa mkono unaotesa ni tashbiha inayomaanisha kuacha kufanya vitu hivyo. "acha kunitesa mimi"

usiache utisho wako unifanye mimi kuogopa.

Tungo "utisho wako" inamaanisha kile kinachosababisha watu kumwogopa Mungu"

Job 13:23

Habari za Jumla"

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa Mungu.

Kwa nini unaficha uso wako kutoka kwangu mimi na kunitendea mimi kama adui yako?

Ayubu anauliza swali hili kulalamika kuhusu jinsi Mungu anavyomtendea yeye. Yeye huenda anategemea jibu.

unaficha uso wako kutoka kwangu mimi

Mtu kuficha uso wake inawakilisha kukataa kumtazama yeye au kumpuuza yeye. Wewe unakaa kunitazama mimi" au " wewe unanipuuza mimi"

Je, wewe utalitesa jani linalopeperushwa

Ayubu anatumia swali hili kumwambia Mungu kuwa Ayubu si wa muhimu na ni dhaifu, ni hasara kumtesa yeye"

jani linalopeperushwa....bua kavu

"Jani" na "bua" ni tashbiha ikielezea udhaifu wa Ayubu, kutokuwa wa muhimu, na kutokuwa mwenye nguvu. "Wewe unanitesa mimi, lakini niko dhaifu kama jani lililopeperushwa na upepo na si wa maana kama bua kavu"

Job 13:26

Habari za Jumla:

Ayubu anamaliza kutoa hoja yake kwa Mungu.

Kwa maana wewe unaandika chini vitu vichungu dhidi yangu mimi;

"Vitu vichungu" vinawakilisha mashitaka. " wewe waandika chini mashitaka dhidi yangu"

wewe unanifanya mimi kurithi uovu wa ujana wangu.

maanza zaweza kuwa 1) kuwa mwenye hatia kwa dhambi za ujana wangu au 2) Kuwa ameadhibiwa kwa dhabi za ujana wake. "wewe waniadhibu mimi kwa dhambi za ujana wangu"

uovu wa ujana wangu.

kielezi cha jina "ujana" kinawezakutafsiriwa pamoja na neno" kijana." "Dhambi ambazo mimi nilitenda wakati nilipokuwa kijana"

Wewe pia unaiweka miguu yangu katika nguo nyembamba

Kufanya hivi kunawakilisha kumwadhibu Ayubu na kumzuia kuishi kwa uhuru kama vile Ayubu ametenda kosa la kihalifu na alikuwa mfungwa. " Ni kama vile wewe unaniweka miguu yangu katika gunia."

nguo nyembamba

Ni kitu ambacho huzuia miguu ya mfungwa kwamba hawezi kabisa kujongea hata kidogo. au ni mnyororo kuzunguka miguu ya mfungwa ambayo humfanya atembee kwa shida. Hivi vimetumika kama ishara ya hukumu.

wewe waangalia njia zangu zote;

Njia huwakilisha vitu ambavyo Ayubu hufanya. " kila kitu ninachokifanya"

wewe wachunguza chini mahali ambapo nyayo za miguu yangu zimekanyaga.

Nyayo za miguu yake vinawakilisha mtu anyetembea " wew wachunguza chini mahali ambapo nimekanyaga"

wewe wachunguza chini mahali ambapo nyayo za miguu yangu zimekanyaga.

Kuchunguza hapa chini kunawakilisha kuchunguza yote ambayo Ayubu amefayafanya. "Ni kama vile ingawa wewe unachunguza chini mahali ambapo nimetembea" au Wewe wachunguza kila kitu inachokifanya kama mtu anavyochunguza nyayo za mtu alizokanyaga chini ya ardhi"

kama kitu kilichooza ambacho hutupwa mbali,

Ayubu analinganisha maisha yake kama kitu kile ambacho kinaoza. Yeye anakufa pole pole.

kama vazi lile ambalo nondo wamelila.

Ayubu anajilinganisha yeye mwenyewe na nguo iliyotoboka toboka kwa sababu nondo wa wamelila sehemu zake.

Job 14

Job 14:1

Habari za Jumla:

Sura hii ni mwendelezo wa hotuba ya Ayubu, iliyoanza 12:1. Ayubu anazungumza kwa Mungu.

Mwanadamu, ambaye amezaliwa na mwanamke,

Sentensi hii ina maanisha watu wote,wanaume na wanawake wote wamezaliwa katika ulimwengu huu.

huishi siku chache tu

hapa imetumika lugha ya kukuza jambo ili kutoa msisitizo kwamba watu huishi muda mfupi tu. " hushi muda mfupi sana"

amejaa mahangaiko.

Kujaaa "mahangaiko" inaonyesha kupata mateso mengi. "yeye ana mahangaiko mengi" au " anateseka sana"

Yeye huchanua kutoka katika ardhi kama ua na kukatwa chini;

Kama maisha ya ua, maisha ya mtu ni mafupi na ni rahisi kuuawa.

yeye hukimbia kama kivuli na hawezi kudumu.

Maisha mafupi ya mwanadamu yamelinganishwa na kivuli ambacho hutoweka haraka.

Je, wewe unatazama chochote katika hivi?

Ayubu ana maanisha kuwa yeye hahitaji Mungu amsikilize sana." Wewe hautazami chochote haya" au " Wewe haunisikilizi sana mimi "

tazama katika hivi

Kumtazama mtu kunawakilisha kuwa makini kumsikiliza ili kumhukumu yeye. "Kuwa tayari kusikiliza" au " tazama makosa ndani yake"

Mnanileta mimi hukumuni pamoja nanyi?

Ayubu anatumia swali hili kuonyesha kushangaa kwake kuwa Mungu anamhukumu yeye ingawa Ayubu si wa thamani kama ua."Lakini wewe wanihukumu mimi"

Job 14:4

Habari za Jumla:

Habari za Jumla: Ayubu anaendelea kuzungumza kwa Mungu.

Ni nani anayeweza kukileta kitu safi kutoka katika kitu kichafu? Hakuna awaye yote.

Ayubu anatumia swali hili kumshawishi Mungu kufanyia kazi kile ambacho yeye anakifahamu kuhusu vitu visivyo safi kwa Ayubu."Hakuna hata mmoja ambaye anaweza kukileta kitu kilicho safi kutoka kwenye kitu kichafu"

Siku za mwanadamu zimeamriwa

"Wewe unaziamuru siku za mwanadamu" au "Wewe unaamua siku za kuishi mwanadamu"

Idadi ya miezi yake unayo wewe;

Idadi ya miezi ya mwanadamu kuwa na Mungu inawakilisha Mungu kuamua idadi ya miezi ambayo mtu ataishi," Wewe waamua ni miezi mingapi yeye ataishi"

umekiweka kikomo chake ambacho hawezi kukivuka

Kuweka kikomo inawakilisha kuishi muda uliopita ambao Mungu ameuweka kwa mtu kufa. "Wewe umeuweka wakati ambao yeye atakufa", na yeye hawezi kuishi zidi ya hapo.

mtu aliyekodishwa

mtu aliyekodishwa kufanya kazi na huenda nyumbani baadaye.

Job 14:7

Kunaweza kuwa na tumaini kwa mti ;

Kielezi cha jina " Matumaini" chaweza kuelezwa pamoja na kitenzi " Tumaini." Tumaini limeelezwa katika mistari 7-9. "Sisi tunaweza kutumaini kuwa mti utaishi tena"

unaweza kuchipua tena

"Unaweza kuanza tena kukua"

hivyo chipukizi lake halitapotea.

Kupotelea mbali kunawakilisha kufa. "ili ya kwamba chipukizi lake halitakufa"

Japokuwa

"Ingawa" au "Hata kama"

shina

sehemu ya mti ambayo hubakia imetokeza nje kutoka ardhini baada ya mti kukatwa sehemu zingine za mti.

hata kama bado lina harufu ya maji

Sentensi hii yaweza kutafsiriwa hivi: shina linalokufa kama ikiwa linaharufu ya maji inawakilisha maji yako karibu nalo." hata kama maji kidogo yako karibu nalo"

litachipua tena

"litaanza kukua"

na kutoa nje matawi kama mche.

mtu kutoa majani inawakilisha matawi kukua katika mti. "na matawi yataanza kukua juu yake kama mche"

Job 14:10

na tena yuko wapi yeye? 11Kama maji

Ayubu anatumia swali hili kusisitiza kuwa wakati mtu anapokufa, yeye ametoweka. na hakuna hata mmoja anayefahamu aliko" au " na yeye ametoweka"

ma maji yanavyopotea kutoka ziwani, na kama vile mto upotezavyo maji na kukauka, vivyo hivyo watu hulala chini na hawaamki tena.

Ukweli kwamba kifo hakiwezi kurudishwa kimelinganishwa na maji ambayo hukauka na hayawezi kurudi.

Kama maji yanavyopotea kutoka ziwani, na kama vile mto upotezavyo maji na kukauka,

Tungo hizi mbili zinaeleza wazo moja na zimerudiwa kutoa msisitizo wa ukweli kwamba kifo ni mwicho.

vivyo hivyo watu hulala chini

Kulala chini kunawakilisha kufa." hivyo watu hufa"

na hawaamki tena

Kuinuka tena kunawakilisha kuishi tena. "na kutoishi tena"

hawataamka wala kuamshwa kutoka katika kulala kwao.

Hizi tungo mbili zinamaanisha kitu hiho hicho na zimetumiwa pamoja kusisitiza kuwa kifo ni mwisho. Kulala kunawakilisha kufa na kuamka kunaakilisha kuishi tena. " watu ambao wamekufa hawataishi tena na kufufunuliwa kutoka katika kifo.

Job 14:13

habari za Jumla:

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa Mungu.

Laiti, kwamba ungenificha mim

Huu ni mshangao kuonyesha kile ambacho Ayubu anataka sana lakini yeye hana matumaini ya hakika kutokea. " Mimi ningependa kwamba wewe ungenificha mimi"

ungenitunza mimi katika siri

"niache mimi nimefungiwa" au " niache mimi nimefichwa"

na kisha kuniita mimi katika fahamu

Kumwita mtu katika ufahamu ni nahau ikimaanisha kufikiri juu yake yeye. " na kisha nifikire mimi" au " na kisha unikumbuke mimi"

Ikiwa mwanadamu akifa, yeye ataishi tena?

jibu la hakika ni "hapana." "Kama mtu akifa, yeye hataishi tena"

Ikiwa hivyo

"hivyo" inamaanisha ufahamu kutoka katika mistari iliyotanguliza. " Kama yeye angeishi tena"

kusubiri kule muda wangu wote wa kuharibika

Maneno "muda wngu wa kuharibika" yanawakilisha muda ambao Ayubu angeharibika." kusubiri muda wangu wote kule ingawa ningeharibika"

mpaka kufunguliwa kwangu kutakapokuja

Kitenzi jina "kufunguliwa" chaweza kuelezwa na kitenzi "kufungua." "hadi hapo nitakapofunguliwa" au mpaka pale wewe utakaponiachilia"

Job 14:15

Habari za Jumla:

Habari za Jumla: Ayubu anaendelea kuzungumza kwa Mungu.

mimi ningekujibu

"Mimi ningeitikia kujibu"

Wewe ungekuwa na shauku ya

Jina " shauku" linaweza kuelezwa pamoja na kitenzi "shauku" au "kutamani." Wewe ungekuwa na shauku" au " Wewe ungehitaji"

ya kazi ya mikono yako.

Hapa mikono ya Mungu inamwakilisha yeye kufanya vitu. Ayubu anajisema mwenyewe kuwa kazi ya mikono ya Mungu. " kwa ajili yangu, ambaye umenitengeneza"

hesabu...na kutunza

Vitenzi hivi viwili kwa pamoja vinaeleza tendo moja."Kwa umakini tunza kwa ajili ya"

nyayo zangu;

Nyayo zinawakilisha maisha yake yeye au kile ambacho yeye anafanya."maisha yangu" au vitu ambavyo mimi huwa navifanya"

Wewe usingejali kumbukumbu ya dhambi yangu...wewe ungeufunga

Mistari hii mitatu inaeleza wazo lilelile na imetumika pamoja kusisitiza ujasiri wake yeye, Mungu angemsamehe yeye.

Wewe usingehifadhi mkoba wa dhambi yangu.

Kutunza mkoba wa dhambi ya Ayubu inawakilisha kufikiri juu ya dhambi yake. "wewe usingetazama dhambi yangu" au "wewe usingefikiri juu ya dhambi yangu"

Uovu wangu ungetiwa muhuri katika mkoba;

Kuutia muhuri uovu katika mkoba inawakilisha kuuficha na kukataa kufikiri juu yake. " Wewe ungekataa kufikiri juu ya uovu wangu kama mtu ambaye huficha kitu fulani katika mkoba"

wewe ungeufunika uovu wangu.

Kufunika uovu kwa kitu ili kwamba usiweze kuonekana ni kufikiri juu yake. "wewe ungeuficha uovu wangu" au " wewe ungeupuuza uovu wangu"

Job 14:18

Habari za Jumla:

Habari za Jumla: Ayubu anaendelea kuzunguza kwa Mungu.

milima huanguka na kuwa si chochote;

"Kuwa si chochote" ni nahau ikimaanisha kuharibiwa kabisa. Tungo hii inafafanua juu ya neno "anguka" na kusisitiza uharibifu. "milima imetupiliwa mbali"

miamba huhamishwa kutoka mahali pake;

"miamba kuporomoka chini kutoka mahali pake"

Kama hivi, ninyi mnavyoharibu matumaini ya mwanadamu.

"mnaharibu tumaini la mwanadamu kama vile..mavumbi ya ardhi"

matumaini ya mwanadamu.

"vitu ambavyo mwanadamu anvitumainia"

Job 14:20

Habari za Jumla:

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa Mungu.

Ninyi daima humshinda yeye,

Neno " yeye" linamaanisha kila mtu" Ninyi daima mnamshinda mwanadamu" au " Ninyi daima mnawashinda watu"

yeye hupita mbali;

Kupita mbali kunawakilisha kufa. " yeye hufa"

Ninyi mnabadilisha uso wake

Maana zaweza kuwa hizi: Maumivu kabla ya kufa humfanya uso wake kuwa angavu, au wakati mtu anapokufa, Mungu huufanya uso wa mtu kuwa tofauti.

kumtuma yeye mbali kufa

Sentensi hii inawakilisha kumsababishia yeye kufa.

na kama wakishushwa chini,

Kushushwa chini ni kuaibishwa. " kama wao wameaibishwa" au " ikiwa watu wakiwaaibisha wao"

Job 15

Job 15:1

Elifazi Mtemani

Hili ni jina la mtu. Watu kutoka temani wanajulikana kama Watemani.

Mtu mwenye hekima anapaswa kujibu kwa maarifa yasiyofaa na kujijaza mwenyewe na upepo wa mashariki?

Elifazi anatumia swali hili la kejeli kumkemea Ayubu. "Mtu mwenye busara hapaswi kujibu kwa maarifa yasiyo na faida wala kujilisha yeye mwenyewe na upepo wa mashariki"

kujijaza mwenyewe na upepo wa mashariki?

Upepo unawakilisha hakuna. Tungo hii inazungumzia mtu anyezungumza maneno yasiyo na maana.Mtu huyu ni kama amejaa upepo. "kujijaza yeye mwenyewe na maneno yasiyo na maana"

upepo wa mashariki?

"upepo wa joto" au "upepo wa jangwani"

Anapaswa kuhojiana na mazungumzo yasiyo na faida au na hotuba ambazo kwa hizo yeye hawezi kufanya mema?

Elifazi anatumia swali hili la kizushi kumkemea Ayubu. " Yeye hapaswi kuhojiana na kwa mazungumzo yasiyo na faida" au "Yeye hapaswi kushindana kwa kutumia maneno yasiyo na faida au kutoa hotuba ambazo mwisho wake ni hasara"

Job 15:4

fifisha

"haribu" au " kutostahilisha"

zuia

"fifisha" au "ondolea mbali"

heshima ya

"tafakari juu ya" au " fikiri juu ya"

uovu wako hufundisha midomo yako;

Sentensi hii yaweza kutafsiriwa hivi: "uovu"kama ulikuwa mwalimu wa midomo ya Ayubu umeelezwa kuwa kama vile midomo inajifunza. Hii ina maana kwamba usemi wake umeathiriwa na uovu wake kwa kiwango kikubwa. "uovu wako ni kama mwalimu na mdomo wako ni kama mwalimu" au " hii ni kwa sababu ya wewe kutenda dhambi kwamba unaongea kama vile wewe unavyofanya"

Mdomo wako

Mstari huu unamzungumzia Ayubu, lakini unarejea kwa "mdomo" wake kutilia mkazo kile anachokisema. "wewe pia wazungumza" au "wewe wasema kile ambacho wewe wasema"

kuwa na ulimi wa mtu mwenye hila

Sentensi hii inarejea jinsi mtu mwenye hila huzungumza kama "ulimi" wake. "kuzungumza katika njia ya mtu mwenye hila"

hila

"udanganyifu"

Mdomo wako mwenyewe hukukukumu wewe, siyo wangu;

Maneno haya yanamwelekea Ayubu na Elifazi kwa "midomo" yao kutilia mkazo kwa kile wanachosema. "Wewe umelaaniwa kwa kile ambacho unakisema, siyo kwa kile ambacho mimi ninachokisema, siyo mimi ninayekulaani wewe"

midomo yako mwenyewe hushuhudia

Ni "midomo" ya Ayubu kuweka msisitizo kwa kile ambacho anakisema. "maneno yako mwenyewe" au "wewe washuhudia"

Job 15:7

habari za Jumla

Kila mstari ni mfano ambao unabeba maswali mawili yenye kejeli .

Je, wewe ni mwanadamu wa kwanza ambaye aliyezaliwa?

Jibu dhahiri ni "hapana" Swali hili la kejeli linaweza kuwekwa katika hali isiyo ya kuuliza: Wewe siyo mtu wa kwanza aliyezaliwa"

Je, wewe ulizaliwa?

"Je, Mungu alikuleta"

Wewe ulikuwepo kabla ya vilima kuwepo?

Jibu sahihi ni "hapana" Hili ni swali la kejeli laweza kuwekawa hivi katika hali isiyo ya kuuliza: Wewe hujaletwa katika dunia kabla ya milima" au " Mungu hakukuleta wewe katika dunia kabla yeye hajaleta vilima katika dunia"

Wewe Umewahi kusikia maarifa ya siri ya Mungu?

Jibu dhahiri ni "hapana" Swali hili la kejeli laweza kuwekwa katika hali isiyo ya kuuliza hivi: "Wewe hujasikia siri za maarifa ya Mungu"

Je, wewe wajihesabia mwenye hekima wewe mwenyewe?

swali hili la kejeli linasisitiza kuwa yeye hawezi kujihesabia hekima yeye mwenyewe. "Wewe huwezi kujihesabia hekima wewe mwenyewe" au " Wewe siyo mtu pekee mwenye hekima"

Ni kitu gani unachokifahamu wewe ambacho sisi hatukijui?

Jibu sahihi ni "hakuna"Hakuna chochote ambacho unakijua ambacho sisi hatukijui" au "Kila kitu unachokifahamu, hata sisi tunakifahamu"

Ni kitu gani unachokifahamu wewe ambacho hakiko katika sisi?

"Kila kitu unachokifahamu , sisi pia tunakifahamu" au "Sisi tunakifahamu kila kitu unachokifahamu"

Job 15:10

Pamoja nasi wapo pia wenye mvi na watu wazee sana

wnye mvi na wazee sana- Elifazi anajiongelea yeye mwenyewe na watu wengine kuwa na hekima ya wazee ambao kwao walijifunza kana kwamba walikuwa pamoja nao katika mwili."Sisi tumepata hekima kutoka pia kwa watu wenye mvi na watu wazee sana"

wenye mvi na watu wazee sana ambao ni wazee

wenye mvi na watu wazeesana-tungo "wenye mvini ufafanuzi wakibinadamu "kwa watu ambao wamezeeka sana" "watu waliozeeka sana wana mvi"

wazee zaidi kuliko baba yako

Hii ni lugha ya kukuza jambo. "mzee kuliko baba yako"

faraja ya Mungu...ni ya upole dhidi yako wewe?

Hili ni swali la uzushi na kejeli ni shitaka lenye tumaini la jibu la "ndiyo"." Swali hili laweza kuweka katika hali isiyo ya kuuliza: Wewe ni sharti ufikiri kwamba faraja za Mungu ni ndogo mno kwako, maneno ambayo ni ya upole kwako.

faraja

"kufariji" au "kuchukuliana"

Job 15:12

Kwa nini moyo wako wewe unakupeleka mbali?

hapa " moyo" unawakilisha hisia za mtu. " kwa nini hisia zako zinakupeleka mbali" au Kwa nini wewe unaruhusu hisia zako kuongoza uamuzi wako?

Kwa nini macho yako yananga'ra

Sentensi hii imaanisha Ayubu kuonekana mwenye hasira Kwa uwazi kabisa muonekano wa mcho yake yeye. " Kwa nini macho yako yanaonekana mwenye hasira" au "Kwa nini wewe unakasirika"

kuirejesha roho yako

hapa neno "roho" linamaanisha utu wote wa mtu. "geuka wewe mwenyewe"

kuyatoa maneno hayo kutoka katika mdomo wako

hapa inamwelezea "yeye akizungumza na hivyo wewe wasema vitu vya kuumiza dhidi yake yeye"

Je, mwanadamu yeye ni nini kwamba yeye anapaswa kuwa safi?

Maswali haya mawili kimsingi ni kitu kimoja na yametumika pamoja kusisitiza kuwa mtu hawezi kuwa mkamilifu"

safi

mtu ambaye Mungu humfikiria kuwa kiroho amekubalika amezungumzwa kama mtu ambaye kimwili alikuwa safi.

mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke ni nini kwamba yeye anapaswa awe mwenye haki?

Swali hili la kizushi limeulizwa kusisitiza kwamba mtu hawezi kabisa kuwa "mkamilifu." Bila kutumia swali sentensi hii yaweza kusomeka hivi: "Mtu aliyezaliwa kutoka kwa mwanamke kamwe hawezi kuwa mkamilifu."

Job 15:15

Tazama

Neno hili limetumika kuvuta usikivu wa Ayubu kwa kile ambacho kimezungumzwa hapo baadaye.

mmoja wake aliye mtakatifu;

"malaika wake yeye"

safi

mtu ambaye Mungu humfikiria kuwa kiroho amekubalika amezungumzwa kama mtu ambaye kimwili alikuwa safi.

machoni pake yeye;

Hapa machoni pake inawakilisha hukumu au tathimini.

mbaya na mla rushwa,

Maneno haya mawili kimsingi yanamaanisha kitu kilekile na linatia mkazo jinsi gani watu walivyo waovu.

ambaye hunywa uovu kama maji!

Sentensi hii inaelezea uovu kama vile ulikuwa maji unayokunywa. Inalinganisha mtu mwovu hutamani kutenda dhambi kwa vile jinsi gani yeye anavyokuwa na shauku ya kunywa maji ya uvuguvugu. "wao wapendao uovu ni zaidi kama vile wanapenda kikombe cha maji ya baridi" au "wao ambao ni kawaida yao kutenda matendo maovu kama wanavyokunywa maji ya baridi"

Job 15:17

Mimi nitakuonyesha wewe;

Hii ni nahau. "Mimi nitakuleza wewe" au " Mimi ninaweka wazi kwako wewe"

Mimi nitakutangazia wewe

"Mimi ntatangaza"

mababu zao hawakuvificha.

Elifazi anasisitiza kuwa mababu zao kwa makusudi waliwafundisha vitu hivi. " mababu zao waliwafundisha wao waziwazi"

Job 15:19

ambao kwao pekee nchi walipewa,

"kwa hao ambao Mungu pekee aliwapa nchi"

miongoni mwao hakuna mgeni aliyepita.

Hii inamaanisha kwamba hakuna mgeni aliyeishi kati yao, kwa uwazi ili kwamba wasiweze kuathiriwa na dini za kipagani. " hakuna mtu awaye yote kutoka katika nchi nyingine aliyekuja na kuwasababisha wao kufikiri vibaya juu ya Mungu"

hupitia katika maumivu

"kuteseka kwa maumivu mengi." Hii yaweza kuwa mayteso ya mwili au kihisia"

idadi ya miaka iliyowekwa juu

"miaka yote ambayo Mungu ameiweka juu"

iliyowekwa juu

Hii ni nahau. "ambavyo vimeandaliwa" au "vile vilivyoweka maalumu"

Sauti ya vitisho katika masikio yake;

"Yeye anasikia sauti za kuogofya siku zote"

Job 15:22

Sentensi Unganishi:

Elifazi anaendelea kumwelezea mtu ambaye ni mwovu anaanza kuelezea katika 15:19.

rudi kutoka katika giza;

Katika sentensi hii "giza" ni tashbiha kuonyesha mahangaiko au mambo mabaya" "epuka mambo mabaya"

Upanga humngojea yeye

katika tungo hii neno " upanga" inawakilisha adui ambaye anangojea kumuua mtu mwovu. Maana zaweza kuwa 1) yeye amehofu kwamba mtu fulani atamchinja yeye" "yeye anahofia kwamba mtu fulani yuko karibu kumwua yeye" au 2) ni dhahiri kwamba yeye anaenda kuuawa. "mtu fulani anamngojea kumtoa uhai"

kwa ajili ya mkate

Sehemu hii "mkate" unamaanisha chakula kwa ujumla" "kwa chakila"

siku ya giza

Hii ni nahau. "siku ya uharibifu" au "kipindi cha kifo chake"

iko mkononi.

Hii ni nahau. "inakuja hivi karibuni"

hushinda dhidi yake yeye,

"zidi nguvu" au "shinda"

kama mfalme tayari kwa vita.

Hii inaliganisha jinsi ukiwa wake na mateso yake makali kumshinda yeye kwa jinsi mfalme ambaye yuko tayari kwa vita, angeshinda dhidi yake. "kama ilivyo kwa mfalme , aliye tayari kwa vita, angeshinda dhidi yake yeye"

Job 15:25

yeye ameunyosha mkono wake dhidi ya Mungu

"yeye ameitikisa mikono yake dhidi ya Mungu." Hii ni ishara ya kukasirika.

hukimbia kwa Mungu

Sentensi hii inamhusu mtu mwovu anatenda kwa hila dhidi ya Mungu kama vile yeye alikuwa akikimbia kumkabili kumshambulia yeye" kumshambulia Mungu" au " kutenda kwa hila dhidi ya Mungu"

kwa vifundo vikubwa vya ngao.

kwa ngao yake yenye nguvu"

Job 15:27

Hii ni kweli,

Sentensi hii inamaanisha mtu mwovu kukimbia kwa Mungu kama ilivyoelezwa kutoka katika mistari iliyotangulia.

yeye amefunika uso wake kwa mafuta yake na amekusanya mafuta juu ya viuno vyake

Mtu huyu mwovu ameelezwa kama mtu mnene kna dhaifu wakati akijiamini mwenyewe kuwa ni mwenye nguvu vya kutosha kumshinda Mungu. "yeye ni dhaifu na uso mnene na viono vilivyowanda.

hakuna mwanadamu anayeishi humo

"ambazo zimetelekezwa"

magofu.

"mabaki" au "majalala"

Job 15:29

Yeye hatakuwa tajiri; utajiri wake yeye hautadumu

"yeye atakuwa masikini, fedha zake zote hazitaonekana"

hata kivuli chake hakitadumu katika nchi.

Sentensi hii inarudia wazo ambalo ni kwamba mali zote za mtu mwovu hazitaonekana."

nje ya giza;

Giza katika sentensi hii linamaanisha kifo. "nje ya giz la kifo"

mwali wa moto utakausha matawi yake;

Katika sentensi hii "mwali wa moto" unawakilisha hukumu ya Mungu na kukauka kwa ghala zake yeye kunawakilisha ukweli kwamba mali zake yeye kupotelea mbali, au kwamba yeye atakufa" Mungu atakitupilia mbali kila kitu ambacho yeye anachokimiliki" kama moto ukaushavyo majani ya mti mbichi"

pumzi ya kinywa cha Mungu

"Pumzi ya Mungu" inawakilisha hukumu yake yeye.

yeye ataenda zake.

Sentensi hii inamaanisha yeye mwenyewe kufa. "yeye atakufa"

Job 15:31

upuuzi utakuwa mshahara wake yeye.

"kwa maana kama yeye ataweka tumaini katika hvitu , upuuzi utakuwa ujira wake yeye"

tawi lake halitakuwa kijani.

Sentensi hii inazungumzia kuhusu mtu kuonekana tofauti na mfu kama vile ilivyokuwa ghala iliyokauka au tawi. " yeye ataonekana mfu, kama vile tawi la mti uliokufa lisivyoonekana kibichi"

Yeye atazipukutisha... yeye atayaondoa

Mistari hii miwili inatoa picha moja ambayo imerudiwa kusisitiza kuwa jambo hili litatokea kwa hakika.

Yeye atazipukutisha zabibu zake zisizovunwa kama kama mti wa mzabibu

Sentensi hii inazungumza juu ya mtu mwovu kuwa dahifu na kufa kama vile alikuwa mti wa mzabibu ukidondosha zabibu ambazo bado kuvunwa. "Kama vile mti wa mzabibu unavyoangushusha zabibu zake ambazo bado kuvunwa, viyo hivyo mtu mwovu atadondosha nguvu zake"

yeye atayaondoa maua yake kama mti wa mzeituni.

Sentensi hii inazungumza juu ya mtu mwovu kuwa dhaifu na kufa kama vile alikuwa mti wa mzabibu ukidondosha zabibu ambazo bado kuvunwa. "Kama vile mti wa mzabibu unavyoangusha zabibu zake ambazo bado kuvunwa, viyo hivyo mtu mwovu atadondosha nguvu zake"

Job 15:34

Kwa maana msaada wa watu wasiomcha Mungu

"kundi la watu wasiomcha Mungu"

moto utateketeza hema za rushwa.

Tungo "hema ya wala rushwa" ina maanisha kuwa watu waovu walizinunua hema hizi kwa pesa walizozipata kwa njia ya rushwa. "hema walizozinunua kwa rushwa zao, zitachomwa kwa moto"

Wao wanabeba mimba yenye ubaya na kuzaa uovu; tumbo lao hutunga mimba ya udanganifu.

Wazo hilihilo limerudiwa mara tatu kutoa msisitizo kwa kiwango gani watu hawa huzalisha waovu. Sentensi hii inamzungumzia mtu ambaye anapanga kufanya vitu viovu, na wanavifanya kama vile mtu aliyekuwa akibeba mimba na kuzaa vitu hivi kama vile mwanamke anavyotunga mimba na kuzaa mtoto. "Wao wanapanga kusababisha mambo maovu ya kitoto na kufanya vitu viovu; daima wao wanapanga kuwadanganya wengine"

tumbo lao hutunga mimba

Katika sentensi hii neno "tumbo" limetumika kumaanisha mtu na kusisitiza kuhusu kutunga mimba, kama ilivyo katika tumbo ambalo utungaji mimba hufanyika humo. "wao wanatunga mimba"

Job 16

Job 16:1

ninyi nyote ni wafariji wenye kuhuzunisha.

"Badala ya kunifariji mimi, ninyi nyote mnanifanya kuwa mwenye kuhuzunika"

Maneno yenye upuuzi daima yanaweza kuwa na mwisho?

Ayubu anatumia swali hili la kizushi kuonyesha kwamba yeye anapenda kwamba wao wangeacha kuzungumza maneno yasiyo na faida. "Jinsi gani mimi ningependa maneno yenu yasiyo na maana yakome.!

Nini kimeharibika kwenu kwamba mnajibu kama hivi?

Ayubu anatumia swali hili la kejeli kumkemea Elifazi. Neno "wewe" linamaanisha Elifazi ambaye amemaliza punde kuzungumza kwa Ayubu. "Elifazi, wewe unapaswa kuacha kunijibu mimi kama hivi"

Job 16:4

Mimi ningekusanya na kuunganisha maneno pamoja

"Mimi ningefikiri vitu vya kuzungumza"

tikisa kichwa changu

Hiki ni kitendo ambacho kinaonyesha kutokukubalika.

katika dhihaka

Neno "mzaha" laweza kuelezwa kama kitenzi "kukudhihaki wewe"

Laiti, jinsi gani Mimi ningewatia moyo na midomo yangu! Jinsi gani faraja kutoka midomo yangu ingenga'risha huzuni yenu!

Hapa Ayubu anazungumza kwa kumaanisha kinyume cha kile anachokizungumza. "Maneno yangu kwa hakika yangekuwa hayawatii moyo ninyi" Wao hakika hawaing'arishi huzuni yako wewe" au " Kwa uzungumza kwako kama mlivyozungumza kwangu hapa manzo, Mimi nisingewatia moyo ninyi au kuinga'risha huzuni yenu"

na midomo yangu!

katika sentensi hii "mdomo" wa Ayubu unawakilisha kile ambacho yeye anasema. "Kwa kile ambachop mimi ninasema"

faraja kutoka midomo yangu

Sentensi hii ina maanisha maneno yenye kutia moyo ambayo anayazungumza. "maneno yangu ya kutia faraja"

ingenga'risha huzuni yenu!

Hapa huzuni imezungumzwa kama ilikuwa mzigo mzito wa mwili. "ingepunguza huzuni yako " au " ingewasaidia kujisikia asiye na huzuni"

Job 16:6

kuomboleza

Ayubu amepitia majonzi mazito ya kupoteza familia yake na afya hiyo ni haielezeki na kwa hiyo, inamsababishia yeye "huzuni kubwa na maumivu ya hisia."

jinsi gani mimi ninasaidiwa?

Ayubu anatumia swali hili la kizushi kueleza kuwa kunyamaza kimya hakupunguzi huzuni yake yeye. Swali hili laweza kuandikwa bila kuwekwa katika hali ya swali. "hainisaidii mimi hata kidogo."

Lakini sasa, Mungu wewe

Ayubu sasa anarudisha lalamiko lake kwa Mungu.

umeifanya familia yangu yote kuwa ukiwa.

"umeharibu familia yangu yote"

Wewe umenifanya mimi kukauka,

Sentensi hii inamaanisha kuwa mwili wa Ayubu umekonda na kuwa na mikunjamano. "Wewe umeufanya mwili wangu kukonda"

ambayo yenyewe ni ushuhuda dhidi yangu mimi

Ayubu anaelezea kukonda kwa mwili wake kama vile ulikuwa kama mshitaki dhidi yake "na watu wanafikiri kuwa unanionyesha mimi kuwa ni mwenye dhambi"

kukonda kwa mwili wangu huinuka dhidi yangu, na kunashuhudia dhidi

Ayubu anaelezea hali ya kukonda kwa mwili wake kama vile ulikuwa mshitaki dhidi yake yeye. "Wote wanaona jinsi mwili wangu ulivyokonda, na wanafikiri hicho kinathibitisha kuwa mimi ni mwenye hatia"

dhidi ya macho yangu.

Hapa Ayubu anazungumzia kwa "uso "wake. "dhidi yangu mimi"

Job 16:9

Mungu amenirarua mimi katika ghadhabu yake na amenitesa mimi; Yeye amenisaga mimi kwa meno yake; Adui yangu amenikazia macho yake juu yangu kama yeye anavyonirarua mimi vipande.

Maneno haya yanazungumza juu ya Mungu kumsababishia Ayubu maumivu kama vile alikuwa mnyama wa porini na Ayubu alikuwa kama mawindo yake alikuwa akiua. Kwa sababu Mungu ana hasira kali na mimi, ni kama vile alikuwa mnyama wa mwituni ambaye anararua mwili wangu vipande vipande kwa meno yake kwa sababu alikuwa adui yangu"

Adui yangu

Sentensi hii inarejea kwa Mungu kama "adui"yake. Inaeleza jinsi yeyey alivyomsababishia yeye maumivu makali.

amenikazia macho yake juu yangu

Hii ni nahau."ananitazama mimi kwa hasira"

Watu wameachama na midomo iliyowazi

"Kuachama" ina maanisha kukazia macho katika mshangao na mdomo ulioachama.

Job 16:11

Mungu amenikabidhi mimi juu ya watu wasio mcha Mungu, na kunitupa mimi ndani ya mikono ya watu waovu

Mistari hii miwiwli kimsingi inamaanisha kitu kilekile. Kwa pamoja inasisitiza hisia za Ayubu za kuwa amesalitiwa na Mungu.

amenikabidhi mimi juu ya

Hii ni nahau. "ameniweka mimi chini ya himaya ya "

kunitupa mimi ndani ya mikono ya

Katika sentensi hii "mikono ya mtu" inamaanisha "udhibiti" wake "amenitoa mimi kwenye udhibiti"

na yeye amenivunjavunja mimi vipande.

Ayubu anazungumza juu ya maumivu yake na kukosa matumaini kama vile yeye alikuwa kitu ambacho kimevunjwavunjwa vipande. . "lakini kisha alikuwa yeye amenivunja mimi vipande vipande.

ameniponda mimi vipande vipande;

Ayubu anazungumza juu ya maumivu yake na kukosa matumaini kama vile yeye alikuwa kitu ambacho kimevunjwavunjwa vipande. " ni kama vile amenichukua mimi kwa shingo na kunivunjavunja vipande"

yeye pia ameniweka mimi juu kama shabaha yake.

Ayubu anajisema mwenyewe kuwa shabaha ya shambulizi la Mungu ikiwa kama Mungu amemweka yeye shabaha kumpiga upinde. "ni kama vile ameniweka mimi juu kama shabaha"

Job 16:13

Wapiga upinde wake wote wamenizunguka mimi;

Ayubu anajisema mwenyewe kuwa shabaha ya shambulizi la Mungu ikiwa kama Mungu amemweka yeye shabaha yake na Mungu alikuwa na wapiga upinde wakimzunguka yeye kumshambulia yeye. "ni kama vile wapiga upinde wake wamenizunguka mimi"

Mungu huzikata vipande vipande figo zangu, na haniokoi mimi; yeye humwaga nje nyongo yangu juu ya ardhi

Ayubu anazungumza juu ya maumivu ambayo yeye anajisikia kwa kuyalinganisha na Mungu kuchoma mwili wake yeye kwa upindeambao anaupiga. Hapa "Mungu "anawakilisha upinde umechoma figo na ini langu mimi, na kuimwaga nyongo yangu juu ya ardhi. Yeye hajanihifadhi mimi"

yeye hukanyaga kanyaga kupitia ukuta

Ayubu anazungumza juu ya maumivu ambayo anahisi kwa kujilinganisha yeye mwenyewe na ukuta ambao Mungu anapita kukanyagakanyaga." "Mimi ninajisikikia kama ukuta ambao kupitia huo Mungu huvunjavunja"

yeye hukimbia juu yangu mimi kama shujaa.

Ayubu anamwelezea Mungu kama askari ambaye anamshambulia yeye. "Ni kama shujaa ambaye hukimbia juu yangu kunishambulia"

Job 16:15

Mimi nimeshona nguo ya magunia juu ya ngozi yangu

"Kwa sababu mimi ninaomboleza, Mimi nimeshona pamoja nguo ya magunia kuvaa kama nguo yangu" au "Mimi navaa nguo ambayo nimeitengeneza kutoka katika magunia kwa sababu ninaomboleza"

Mimi nimeisukuma kwa nguvu pembe yangu ndani ya ardhi.

"Pembe" ya Ayubu inawakilisha nguvu na mamlaka aliyokuwa nayo kabla lakini sasa haipo tena. " Mimi nina simama hapa katika uchafu, mkiwa sana."

juu ya ngozi inayofunika macho kuna kivuli cha mauti

"kuna giza linazunguka macho yangu" au " macho yangu yana giza, kama jicho lamtu aliyekufa"

hakuna dhuluma katika mikono yangu,

"Mikono" inamaanisha uwezo wa mtu na utendaji kazi wake. "Mimi sijatenda kwa hila"

Job 16:18

Nchi, haifuniki juu damu yangu mimi

Ayubu anazungumza kwa " nchi"moja kwa moja japokuwa haiwezi kumsikia yeye, kutilia mkazo kwenye hoja yake. Nchi imepewa sifa za kutenda kama binadamu kuifunika juu damu yake baada ya yeye kufa. "Mimi ningependa damu yangu ilowane ndani ya ardhi lakini hiyo ingebaki juu ya ardhi kama uthibitisho wa jinsi nilivyokufa"

Nchi, haifuniki juu damu yangu mimi

Ayubu anajisema yeye mwenyewe akifa kama vile yee angechinjwa . "Damu" yake ni mfano kuonyesha kifo chake yeye. "Nchi, wakati nikifa , usifiche jinsi nilivyokufa visivystahili" au"na isiwe imefichika jinsi ninavyokufa isivyostahili"

acha kulia kwangu kuwe hakuna mahali pa kupumzika.

Ayubu anazungumzia juu ya kumtaka kila mmoja kujua kile kilichotoke kwake yeye kama "kilio" chake alikuwa mtu ambaye hakuacha kamwe kushuhudia kile ambacho kilitokea kwake yeye na hakupumzika kamwe. "Acheni kila mmoja asikie kuhusu kile ambacho kilitokea kwangu mimi"

tazama

Ayubu anatumia neno hili kuvuta usikivu kwa kile ambacho yeye anachokisema baadaye. "sikilizeni"

ushuhuda wangu uko mbinguni

Ayubu anatumaini kuwa mtu fulani atazungumza juu yake kwa Mungu.

ashuhudiaye

"hushuhudia"

yuko juu

Hii ni nahau. "mbinguni" au "juu mbinguni"

Job 16:20

wananicheka

"cheka au kejeli"

jicho langu linamwaga machozi

Ayubu anaeleza jinsi yeye anavyojisikia mwenye huzuni. Katika sentensi hii anaelezea kwa kulikuza jambo la jinsi gani mara nyingi machozi humwagika kutoka katika macho yake. "macho yangu yamejaa machozi wakati mimi ninapolia kwa sauti"

kwa ajili ya mtu huyu

Katika sentensi hii Ayubu anajisema yeye mwenyewe katika nafsi ya tatu"kwa ajili yangu mimi"

kama mwanadamu afanyavyo na jirani yake.

"Ayubu anaeleza jinsi anavyotaka yeye kwamba mmoja mbinguni kumwombea yeye.

mtu huyu

Ayubu anajisema yeye mwenyewe.

Mimi nitakwenda mahali

Pia katika sentensi hii Ayubu anajisema yeye mwenyewe anakufa. " Mimi nitakufa na kwenda mahali"

Job 17

Job 17:1

habari za Jumla:

Ayubu anaendelea kuzungumza.

Roho yangu imemezwa

Ayubu anajisema yeye mwenyewe kwa "roho" yake kusisitiza juu ya hisia zake za ndani. Anazungumza juu ya kukosa nguvu hata kidogo kama kitu ambacho kimetumika. " Mimi nimemezwa" au "mimi nimepoteza nguvu zangu zote"

siku zangu zimekwisha;

Ayubu anarejea kuhusu maisha yake "kama siku zake" muda wangu umekwisha" au " Mimi ninakwenda kufa hivi karibuni"

kaburi lipo tayari kwa ajili yangu mimi.

Tungo hii inaeleza "kaburi" kama vile ni mtu ambaye atampokea Ayubu kama mgeni. "nitakufa hivi karibuni na nitazikwa"

Hakika kuna wenye mzaha pamoja nami

"Wale wanaonizunguka mimi wananidhihaki mimi"

Hakika

"haswa"

ni lazima daima jicho langu litazame

Ayubu anajisema yeye mwenyewe kwa "macho yake" kusisitiza kile ambacho anakiona" Mimi ni lazima daima nione " au "Mimi ni lazima daima nisikie"

kukasirisha kwao

"kusimanga kwao" neno "kukasirisha kwa" laweza kuelezwa kama kitenzi. "wao wananikasirisha mimi" au "wa, wanajaribu kunifanya mimi nikasirike"

Nipe sasa ahadi, uwe uthibitisho kwangu mimi pamoja na wewe mwenyewe;

Hapa Ayubu anaanza kuzungumza na Mungu.Katika Sentensi hii yeye anazungumzia hali yake kama vile alikuwa gerezani. Anamwomba Mungu kutoa msamaha ili ya kwamba yeye aweze kufunguliwa."Mungu, toa sasa msamaha ili kwamba mimi nipate kufunguliwa kutoka katika gereza hili" au " lipa kwa ajili ya kufunguliwa kwangu mimi kutoka gerezani"

nani mwingine yuko pale ambaye atanisaidia mimi?

Ayubu anatumia swali hili la kejeli kusisitiza kwamba hakuna mwingine awaye yote wa kumsaidia yeye. Swali hili laweza kuandikwa bila hali ya kuuliza ikasomeka hivi" "hakuna mwingine awaye yote ambaye atanisaidia mimi"

Job 17:4

habari za Jumla:

Ayubu anaendelea kuzungumza.

umeitunza mioyo yao

Neno "yao" linamaanisha rafiki zake yeye. Wao wamesemwa kwa "mioyo yao" kusisitiza hisia zao."umewatunza wao" au "umewatunza rafiki zangu mimi"

hautawaheshimisha wao juu yangu mimi.

"wewe hautawaruhusu wao kushinda juu yangu"

Yeye ambaye

"Mtu yeyote ambaye"

huwapinga rafiki zake hadharani, kwa ajili ya tuzo

"kwa uongo anawashitaki rafiki zake kwa ajili ya kupata faida" au "huwasaliti rafiki zake ili kupokea tuzo"

macho ya watoto wake yatashindwa kuona.

Watoto wa mtu wamesemwa hapa kwa "macho yao." Tungo hii inawaelezea watoto wanateseka kwa sababu ya kile ambacho baba zao au mama zao walifanya. " watoto wake watateseka kwa ajili yake"

Job 17:6

Habari za Jumla:

Ayubu anaendelea kuzungumza.

amenifanya mimi kuwa neno la kuzungumziwa na watu;

Sentensi hii ina maanisha kwamba watu wanasema juu yake kwa kumkejeli na kulitumia jina lake kama masimango."kwa sababu yake yeye mwenyewe, watu hutumia jina langu kama masimango" au "kwa sababu yao, watu hutumia jina langu kama neno la kuzungumzwa na watu"

wao wananitemea mate katika uso wangu mimi.

"watu hunitemea mate usoni pangu" Katika utamaduni huu kumtemea mate mtu usoni ilikuwa ni dhihaka kubwa. "watu hunisimanga mimi sana , kwa kunitemea mate mimi usoni pangu"

jicho langu pia halioni vizuri kwa sababu ya huzuni;

Mungu nazungumza juu y uoni wake kama "macho yake" "Kuona kwangu kumefifia kwa sababu Mimi nina huzuni sana" au "Mimi ni kipofu kabisa kwa sababu ya huzuni yangu"

sehemu zangu zote za mwili wangu ni nyembamba kama kivuli

Kivuli hakina wembamba.Hii ni lugha iliyokuzwa kwa kuonyesha jinsi gani sehemu za mwili wa Ayubu zilivyokuwa nyembamba.

sehemu zangu zote za mwili

Huu ni mjumuisho uliotumiwa kusisitiza kuwa mwili wake wote ni mwembamba, lakini ina maanisha kwa uwazi zaidi mikono yake na miguu yake. "mikono yangu na miguu yangu"

watashtushwa

"tiwa mshtuko" fadhaishwa"

kwa hiki

"kwa kile ambacho kimetokea kwangu mimi"

atajitia yeye mwenyewe juu ya kushindana dhidi

Hii ni nahau. "wata kuwa wametiwa hofu kwa sababu ya" au" wao watakasirihwa sana na"

Job 17:9

Habari za Jumla:

Ayubu anaendeleza kuzungumza.

ataendelea katika njia yake;

Hii ni nahau. "ataendelea kuishi katika njia ya haki"

yeye ambaye ana mikono iliyo safi

Sentensi hii inazunguza juu ya mtu kuwa asiye na hatia kama mikono iliyo safi. "yeye ambaye hutenda haki" au "yeye ambaye hana hatia"

ataendelea kuwa mwenye nguvu zaidi na zaidi

Maneno haya hayamaanishi tu nguvu za kimwili lakini pia nguvu za utashi wa mtu na hisia.

ninyi nyote

Ayubu anazungumza kwa Elifazi, Bildadi, na Sofari.

njooni sasa

Ayubu anawakaribisha rafiki zake kuhojiana kile ambacho amekisema. "njoni sasa, mhojiane na mimi"

Job 17:11

habari za Jumla:

Ayubu anaendelea kuzungumza.

Siku zangu zimepita

Hii ni nahau. "Muda wangu umepita" au "Maisha yangu yamefikia mwisho"

mipango yangu imenyamazishwa

"mipango yangu kamwe haitatokea" au "mipango yangu kamwe haitatimizwa"

na hivyo ni matumaini

Katika sentensi hii "moyo" wa Ayubu unamaaanisha shauku yake kubwa. "Kama kwa vitu ambavyo mimi nimevionea shauku zaidi"

ya moyo wangu

Katika mstari huu Ayubu hakukamilisha maneno yake kuonyesha kuwa hakuwa na tumaini lolote kwa shauku yake. "kwa moyo wangu, hakuna tumaini lolote la hayo kutokea"

Watu hawa, wenye kukejeli,

Hizi ni tungo mbili zinamaanisha watu wale wale wanoitwa rafiki za Ayubu, Elifazi, Bildadi, na Sofari.Tungo ya pili inasisitiza mtazamo wao usio wa kirafiki.

badili usiku kuwa mchana;

Sentensi hii inazungimzia watu wanaodai kuwa usiku ni mchana kama vile kweli wameubadili usiku kuwa mchana."wao wanadai kuwa huu ni muda wa mchana wakati ni usiku" au "kile wanachosema ni kinyume cha ukweli kama vile usiku ulivyo kinyume na mchana"

mchana uko karibu kuwa giza.

"wanadai kuwa nuru iko karibu na giza" au "wanadai kwamba wakati inapokuwa usiku, hiyo inakuwa mchana"

Job 17:13

Habari za Jumla:

Ayubu anaendelea kuzungumza.

mimi nitazame katika Kuzimu kama nyumbani kwangu;

"Kutazama" ina maanisha "kufikiri" kwa jinsi hiyo. Mimi ninafikiri juu ya kuzimu kama nyumbani kwangu" au "Mimi sasa nafikiri kuzimu ni nyumbani kwangu mimi"

Mimi nimetandaza kiti changu katika giza;

Sentensi hii ina maanisha Ayubu kuwa amejiandaaa kufa kama vile kuwa amekitandika kitanda chake yeye katika giza." "nimejiandaa mwenyewe kwenda na kulala miongoni mwa waliokufa"

nimetandaza kiti changu

"nimekitengeneza kitanda changu"

Mimi nimesema na shimo....na kwa funza,

Mistari hii miwili inatofautiana na imetumiwa kwa pamoja kusisitiza jinsi gani Ayubu alikuwa mkiwa"

shimo

"kaburi"

Wewe ni baba yangu

Ayubu anazungumzia ule ukaribu atakaokuwa nao hivi karibuni na kaburi lake akilinganisha na ukaribu wa mtu alio nao na familia yake"wewe uko karibu na mimi kama baba yangu" au"Wakati mimi nitakapozikwa, wewe utakuwa karibu na mimi kama baba"

funza

"wadudu wadogo." minyoo ambayo ni viumbe wadogo ambao hula miili iliyooza.

Wewe ni mama yangu au dada yangu;

Ayubu anazungumzia ule ukaribu atakaokuwa nao hivi karibuni na kaburi lake akilinganisha na ukaribu wa mtu alio nao na familia yake"wewe uko karibu na mimi kama mama yake na dada zake. "Wew uko karibu na mimi kama mama yangu na dada yangu" au"Wewe utakuwa karibu na mimi kama mama au dada"

liko wapi tena tumaini langu?

Jibu dhahiri ni "hakuna popote," kwa sababu hana tumaini. Swali hili la kejeli linaweza kuandikwa pasipo kutumia swali hivi: "Mimi sina tumaini"

Kama kwa tumaini langu, nani awezaye kuona chochote?

Swali hili la kizushi limetumika kusisitiza kuwa hakuna mtu yeyote anayetarajia yeye kuwa na tumaini lolote. Swali hili la kejeli linaweza kuandikwa bila kutumia swali hivi: "hakuna awaye yote anayeweza kuona tumaini kwangu" au "Hakuna ategemeaye mimi kuwa na tumaini lolote"

Job 18

Job 18:1

Habari za Jumla:

Tazama uandishi wa ushairi na mifano

Habari za Jumla:

Bildadi Mshunami anazungumza kwa Ayubu.

Ndipo Bildadi Mshuhi alijibu na kusema

"Bildadi" ni jina la mtu ambaye ni mmoja wa watu wa kabila la Shua.

Je, lini utaacha kusema kwako

Hili swali la kizushi lina maanisha kuwa Ayubu amekuwa akizungumza kwa muda mrefu. Swali hili la kejeli linaweza kuandikwa bila kutumia swali hivi: "Acha kuzungumza!"

Fikiri,

"Kuwa mwenye kufikiri"au" tafakari juu ya vitu hivi"

Job 18:3

Habari za Jumla:

Bildadi anaendelea kuzungumza kwa Ayubu.

Kwa nini sisi tumehesabiwa kama wanyama

Bildadi anatumia swali hili la kejeli kusisitiza kwa Ayubu kuwa hapaswi kufikiria kuwa ni mpumbavu. Yeye anazungumzia wao kufikiriwa kuwa ni wapumbavu kwa kuwaita "wanyama hatari wa porini." Swali hili laweza kuandikwa billa hali ya kuuliza ikasomeka hivi: Wewe hupaswi kufikiri kuwa sisi ni wanyama hatari wa porini." au "Wewe hupaswi kufikiri kuwa sisi ni wapumbavu kama wanyama"

Kwa nini sisi

Neno "sisi" huenda lina maanisha Bildadi na rafiki wengine wa Ayubu.

kwa nini tumekuwa wapumbavu machoni pako?

Bildadi anatumia swali hili la kejeli kwamba yeye hapaswi kuwafikiria wao kuwa ni wapumbavu."Sisi hatuko wapumbavu kama wewe unavyofikiri kuwa tuko hivyo"

machoni pako?

Katika sentensi hii neno uoni linawakilisha hukumu au tathimini. "katika hukumu yako"

Wewe ambaye wajirarua mwenyewe katika hasira yako

hapa Bildadi anasema kwamba ni kwa sababu ya hasira ya Ayubu na kutokuwa mtiifu kwa hiyo amejeruhiwa, siyo kwa sababu ya hasira ya Mungu kama vile alivyodai hapo kabla. Neno "rarua" hapa linamaanisha "jeruhi" "Wewe umesababisha kujeruhiwa kwako kwa sababu ya hasira"

nchi haipaswi kuachwa kwa ajili yako au miamba inapaswa kuondolewa kutoka mahali pake?

Swali hili la kizushi linasema kwamba kumwacha Ayubu ambaye wanamfikiria kuwa ni mtu mwenye hatia, aende kwa uhuru itakuwa kama kuubadilisha ulimwengu wote. Ayubu anatumia lugha ya kukuza sana jambo jinsi gani inavyoshangaza waanavyofikiri jinsi iliyo. Swali hili laweza kuandikwa billa hali ya kuuliza ikasomeka hivi: Kumwomba Mungu akuache wewe, mtu mwenye hatia, uende kwa uhuru ni kama upumbavu, kama kuiomba ardhi kusamehewa kwa faida yako au kwa ajili ya Mungu kuhamisha miamba kutoka mahali pake kukufurahisha wewe"

nchi inapaswa kusamehewa

"kila mmoja anapaswa kuiacha nchi"

miamba inapaswa kuondolewa kutoka mahali pake?

Neno "mwamba" katika sentensi hii lina maanisha miamba mikubwa, kama vile milima. "Mungu anapaswa kuihamisha milima kutoka mahali pake " au"Mungu aihamishe milima inayozungunguka mahali pale"

Job 18:5

habari za Jumla:

Bildadi anaendelea kuzungumza kwa Ayubu.

Ni dhahiri, nuru ya watu waovu itawekwa nje; cheche ya moto wake haitanga'ra.

Bildadi anazungumza juu ya mtu mwovu kufa kama vile taa yake ilikuwa imewekwa nje. "Kitakachotokea ni kwamba maisha ya watu waovu kama wewe hutoweka haraka kama vile tunavyoweka nje taa au kuzima mwali wa moto"

itawekwa nje;

"itaenda nje"

Nuru itakuwa giza katika hema yake; taa yake juu yake yeye itawekwa

Bildadi anaendelea kuzungumza juu ya maisha ya mtu mwovu kama vile yalikuwa kama mwanga katika hema yake. Itakuwa kama mwanga katika hema yake imerudishwa katika giza, kama taa juu yake iliyozimika.

Job 18:7

habari za Jumla:

Bildadi anaendelea kumwelezea mtu mwovu.

Hatua za nguvu zake yeye zitafanywa kuwa fupi;

maneno haya yanamhusu mtu mwovu ghafla anapatwa na janga kama vile yeye hakuwa na nguvu za kutembea. "Itakuwa kama yeye hakuwa na nguvu za kutembea"

mipango yake yeye mwenyewe itamwangusha yeye chini.

"Ushauri wake mwenyewe unamfanya yeye kuanguka chini." maneno haya yanamzungumzia mtu mwovu akipitia majanga kama vile anavyoanguka chini. "mipango yake yeye mwenyewe itamwongoza yeye katika janga"

Kwa maana yeye atatupwa katika mtego kwa miguu yake mwenyewe; yeye atatembea katika mahangaiko.

"Miguu yake mwenyewe itamwongoza katika mtego." Bibldadi anatumia picha hii kusema kwamba njia ambayo mtu mwovu anaishi maisha yake inamwongoza yeye katika janga la ghafla. " Itakuwa ingawa amejiongoza mwenyewe katika mtego, kama vile yeye alitembea katika mahangaiko"

mtego

ni nguo au kamba ambayo watu huunganisha pamoja kutengeneza kizuio. Watu walitumia mitego kunasa wanyama.

shimo la mahangaiko.

shimo lina matawi na majani juu yake ili kwamba mnyama atapita juu ya matawi yake na majani na kuanguka ndani ya shimo.

Job 18:9

habari za Jumla:

Bildadi anaendela kuzungumza na anatumia picha ya mifano mitatu kuelezea jinsi gani mtu mwovu ghafla atapitia kwenye majanga.

Tanzi litamchukua yeye...mtego utabaki ...Tanzi ime... kwa ajili yake.... katika njia

Tungo hizi nne zinazungumza juu ya mtu mwovu anayepitia majanga kama vile alikuwa amekamatwa na mtgo. "Itakuwa kama mtego utamchukua yeye...mtego uta....Tanzi ina....na mtego kwa ajili yake katika njia"

Tanzi

Watu walitumia aina hii ya mtego kukamata ndege. Mtego umenasa na kufunga na kushikilia kwenye miguu ya ndege.

litamchukua yeye kwa kisigino;

Katika sentensi hii "kisigino" kinamaanisha mguu wote" utaushikilia mguu wake"

Tanzi limefichwa kwa ajili yake chini ya ardhi;

"Mtu fulani ameficha mtego katka ardhi ili kumkamata yeye"

mtego

kamba yenye tundu ambalo hushikilia mguu wa wanyama wakati mnyama anapotembea katikati ya tundu.

na mtego kwa ajili yake

"na mtego umefichwa katika njia kumkamata yeye" au" na mtu fulani atauficha mtego kumkamata yeye katka njia"

Watishao watamfanya yeye aogope juu ya sehemu zote

"watishao wote wanaomzunguka watamfanya yeye aogope"

watamkimbiza yeye kwenye visigino vyake.

Sentensi hii inazungumzia vitu ambavyo vitamfanya mtu mwovu aogope kama vile kulikuwa na adui zake ambao walimfukuza yeye"

Job 18:12

Habari za Jumla:

Bildadi anaendelea kumwelezea mtu mwovu.

Utajiri wake utageuka kuwa njaa,

Maneno haya yanamzungumzia mtu mwovu atakuwa maskini na mwenye njaa kwa kuwa utajiri wake umerudishwa kuwa kitu kingine. "Badala ya kuwa na utajiri, yeye atakuwa maskini na mwenye njaa"

na majanga yatakuwa tayari upande wake.

Maneno "tayari" na kuwa upande wake" ni nahau inayomaanisha kuwa kitu fulani kinaendelea sasa. "na yeye ataendelea kupitia majanga" au "na yeye hataweza kuyaepuka majanga"

sehemu za mwili wake zitakuwa zimemezwa

Pia maneno haya yanazungumzia ugonjwa unaoharibu mwili kama vile ulikuwa mnyama ambaye amemshambulia yeye na alikuwa akimla yeye. Ugonjwa utakula pale katika mwili wake" au " Ugonjwa utaharibu ngozi yake"

mzaliwa wa kwanza wa kifo atazila sehemu zake yeye.

Katika sentensi hii ugonjwa umelinganishwa na "mzaliwa wa kwanza wa kifo." Kusema ugonjwa unaoharibu mwili wake kama vile ulikuwa mnyama ambaye amemshambulia yeye na alikuwa akimla yeye. "ugonjwa hatari utaharibu sehemu tofauti tofauti za mwili wake"

Job 18:14

habari za Jumla:

Bildadi anaendelea kumwelezea mtu mwovu.

Yeye ameraruliwa kutoka kwenye usalama wa hema yake

"Majanga yamemtoa yeye kutoka katika hema yake, mahali ambapo yeye alikuwa salama"

hakuweza kutembea

"na hakuweza kutembea" au"ilimlazimu yeye kuondoka"

mfalme mwenye utisho.

Hili ni rejeo kwa "Mfalme Kifo'" mungu mpagani ambaye alikuwa ameaminiwa kutawala juu ya kifo" "mmoja ambaye anatawala juu ya waliokufa" "mfalme wa kifo"

Watu ambao siyo wa kwake

"watu ambao si wa familia yake"

baada ya kuona ule moto umesambaa ndani ya nyumba yake yeye

Watu walitumia kemikali ya salfa kujikinga na magonjwa yoyote kutoka kwa mgonjwa anayekufa. "baada ya kumwaga kemikali ya salfa juu ya nyumba yake yote"

Job 18:16

Habari za Jumla:

Bildadi anaendelea kumwelezea mtu mwovu.

Mizizi yake itanyauka juu yake ... tawi lake litakatwa.

Sentensi hii inamzungumzia mtu mwovu kufa bila kuwa na uzao kama vile mti ambao mzizi wake umekauka, na matawi kusinyaa na hayatoi matunda. "Yeye atakufa na hataacha uzao, yeye atakuwa kama mti ambao mizizi yake imekauka na ambao matawi yake yote yamenyauka"

tawi lake yeye litakatwa.

""matawi haya yatanyauka"

kumbukumbu lake yeye litapotea kutoka katika nchi; yeye hatakuwa na jina katika mtaa.

Tungo hizi zinabeba maana moja na zimetumiwa pamoja kusisitiza ukweli kwamba hakuna mtu ambaye atamkumbuka yeye baada ya yeye kufa"

Kumbukumbu lake yeye litapotea kutoka katika nchi

Maneno haya yametafsiriwa hivi: "kumbukumbu" za mtu mwovu kama vile zilikuwa mtu aliyekufa" "Hakuna hata mmoja katika nchi ambaye atamkumbuka yeye"

hatakuwa na jina katika mtaa.

Hii ni ni nahau: "hakuna hata mmoja atembeaye katika mtaa atakayeweza hata kukumbuka jina lake yeye"

Job 18:18

habari za Jumla:

Bildadi anaendelea kumwelezea mtu mwovu.

Yeye atafukuzwa kutoka katika nuru mpaka kwenye giza na kuwa amefukuzwa nje na ulimwengu huu

maneno haya pamoja yanasisitiza ukweli kuwa mtu mwovu atapelekwa kuzimuni, mahali pa waliokufa.

Yeye atafukuzwa kutoka katika nuru mpaka kwenye giza

"Mungu atamfukuza mtu mwovu kutoka kwenye nuru kwenda kwenye giza"

na kuwa amefukuzwa nje na ulimwengu huu.

Sentensi hii inamaanisha Mungu kumfanya yeye aiache nchi na kwenda mahali ambapo watu waliokufa huenda. Na kama vile alikuwa kama akimfukuza yeye" "na M ungu atamfanya yeye kuuacha ulimwengu" au Mungu atampeleka yeye mahali ambapo watu waliokufa huenda"

amefukuzwa nje

"Mungu atamfukuza yeye"

Hatakuwa na mtoto wa kiume wala mjukuu miongonni mwa watu wake, wala kizazi chochote kitakachobakia mahali alipokuwa amekaa.

Kwa pamoja tungo hizi zinasisitiza kuwa yeye hatakuwa na familia au uzao ulioachwa"

mtoto wa mtoto wa kiume

"mjukuu"

uzao

"ndugu"

Wale wanaoishi upande wa magharibi watakuwa wametiwa hofu kwa kile kitakachotokea kwake siku moja; wale wanaoishi upande wa mashariki watakuwa wameogopeshwa kwa hicho.

Maneno "upande wa magharibi" na "upande wa mashariki" yote kwa pamoja yanamaanisha watu wote wanaoishi kila mahali. Lugha ya kukuza jambo imetumika kila mtu kaitka nchi atasikia kuhusu kile kilichotokea kwa mtu mwovu anayejulikana. "Kila mtu katika ulimwengu atashtushwa na kushangazwa wakati watakapoona kilichotokea kwa mtu mwovu." au"watu wengi wanaoishi upande wa mashariki na upande wa magaharibi watashtushwa na kushangazwa wakati watakapoona kinachotokea kwa mtu mwovu"

siku moja;

"siku fulani"

Job 18:21

Habari za Jumla:

Bildadi anazidi kumzungumzia mtu mwovu.

nyumba za watu wasio haki, ni sehemu ya wale wasiomjua Mungu

Tungo hizi mbili zina maana moja kwa watu walewale. Katika sentensi hii watu hawa wamezungumzwa kwa mahali ambapo wao wanaishi. "watu wasio haki, wale ambao hawamfahamu Mungu"

Job 19

Job 19:1

Sentensi Unganishi:

Ayubu anazungumza kwa rafiki zake watatu.

Habari za Jumla

Tazama uandishi wa ushairi na mifano ya miti wa mitini

mpaka lini mtanifanya mimi kuteseka na kunivunja vunja mimi vipande vipnde kwa maneno?

Ayubu anatumia swali hili kulalamika kuhusu jinsi rafiki zake wanavyomtemdea yeye. "Acheni kunifanya mimi niteseke na kunikatakata mimi vipande vipande kwa maneno."

kunivunja vunja mimi vipande vipande

Ayubu anatumia picha hii kusema kwamba maneno yao yanamfanya yeye ajisikie mwenye huzuni sana na asiyekuwa na tumaini. "na kunitesa kwa maneno"

Job 19:3

Habari za Jumla:

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa rafiki zake.

Mara kumi hivi mmenishutumu mimi

Tungo "Mara kumi hivi" inamaanisha jinsi ambavyo rafiki zake wamemkemea kabisa Ayubu"Ninyi mmenidhihaki mimi" au" Ninyi mmenidhihaki mimi mara nyingi"

ninyi hamuoni aibu kwamba mmenitendea mimi kwa ukatili.

Ayubu anawakemea wao hivi. "Ninyi mnapaswa kuona aibu kwamba mmenitendea mimi kwa ukatili"

mmenitendea mimi kwa ukatili.

"mmenikejeli mimi"au "mmenidhihaki mimi hadharani"

nimekosa,

"nimetenda dhambi kwa bahati mbaya" au" kwa kufanya makosa nimetenda dhambi"

makosa yangu

"dhambi yangu" au" makosa yangu"

makosa yangu hubaki kuwa wajibu wangu.

Ayubu anamaanisha kwamba rafiki zake hawapaswi kuendelea kumdhihaki yeye" makosa yangu ni juu yangu mimi mwenyewe, hivyo hampaswi kuendelea kunikemea mimi" au " makosa yangu hayakuwaumiza ninyi, hivyo hampaswi kuendelea kunikekemea mimi"

Job 19:5

habari za Jumla:

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa rafikiz ake watatu.

Kama ni dhahiri ninyi mtajiinua juu yangu mimi

"Kama mnafikiri ninyi ni bora kuliko mimi" au" Kwa maana mnatenda kana kwammba ninyi ni bora kuliko mimi nilivyo"

na kuutumia uvumilivu wangu kunipinga mimi

"na kudai kuwa uvumilivu wangu ushahidi dhidi yangu" au"na kuutumia uvumilivu wangu kama ushahidi kwamba mimi ni mwenye hatia"

kuutumia uvumilivu wangu kunipinga mimi

Jina dhahania "uvumilivu" laweza kuelezwa pamoja na kitenzi"vumilia". "dai kwamba kile ambacho kimetokea kwangu kinathibitisha kwamba mimi ni mwenye hatia"

amenikamata mimi katika mtego wake yeye.

Ayubu anazungumza kama Mungu alikuwa mwindaji ambaye amemnasa Ayubu katika mtego wake. Tashbiha hii inamwakilisha Mungu akichukua udhibiti wa hisia za Ayubu za kukosa tumaini. "ameninasa mimi" au "amechukua udhibiti wangu mimi" au" anadhibiti kile kinachotokea , hivyo mimi sina msaada"

Job 19:7

Habari za Jumla:

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa rafiki zake watatu.

Tazama,

Neno hili "Tazama" linatia mkazo unaofuata."Haswa"

dhuluma!"

Hiki ni kilo cha ajili ya msaada. "dhuluma! Msaada! Mimi nimekuwa nikishambuliwa!"

Mimi ninaita kwa ajili ya msaada,

Mimi ninapiga kelele kwa ajili ya msaada" "Ninalia kwa ajili ya msaad"a

lakini hakuna haki.

Jina dhahania "haki"linaweza kutafsiriwa katika tungo hivi: "lakini hakuna hata mmoja anayenilinda mimi kutoka kwa hao wanaotenda mabaya kwangu"

Yeye ameiwekea ukuta .... giza katika njia yangu

"Mungu ameweka ukuta katika njia ambayo kwayo Mimi ninapita juu yake" au "Yeye ameifunga njia hivyo siwezi kuendelea kupita"

Yeye ameiwekea ukuta njia yangu, ili kwamba mimi nisiweze kupita, na yeye ameweka giza katika njia yangu

Ayubu anatumia picha hii kusema kwamba Mungu amemfanya yeye kujisikia kukosa msaada na bila tumaini.

Yeye ameniondoa Mimi kutoka katika utukufu wangu

Ayubu anatumia picha hii kusema kwamba Mungu amechukua heshima yake njema, mali, na mafanikio mbali kutoka kwake.

Yeye ameniondoa Mimi kutoka katika utukufu wangu

Ayubu anazungumza juu ya uttukufu wake kana kwamba kulikuwa na mwizi yule Mungu.

ameichukua taji kutoka kwenye kichwa changu mimi

Taji inaashiria utu wa Ayubu au heshima. "yeye ameiondolea mbali taji ya kichwa changu"

Job 19:10

Habari za Jumla:

Ayubu anaendeleza kuzungumza kwa rafiki zake watatu.

Yeye amenivunjavunja mimi chini kwa kila upande,

Ayubu nazungumza juu ya Mungu akimharibu yeye kana kwamba alikuwa jengo ambalo Mungu analiangusha chini. "Yeye ameniharibu mimi kwa njia zote" au amenishambulia mimi katika nia zote"au "amenishambulia mimi katika kila njia"

na Mimi nimetoweka

Kuwa" umekwenda"linawakilisha kuharibiwa kabisa. "na mimi nimeharibiwa kabisa"

yeye amelikokota juu tumaini langu kama mti.

Ayubu anazungumza juu ua Mungu kusababisha Ayubu kukosa tumaini kana kwamba Ayubu alikuwa mti, Mungu ameukokota mti wote na mizizi yake kutoka katika ardhi. ""yeye ametupilia mbali tumaini lake lote"au " kw sababu ya kile ambacho yeye amefanya, Mimi siwezi tena kutumaini kitu chochote kizuri"

yeye pia ameiongeza ghadhabu yake dhidi yangu mimi

Ayubu anazungumza juu ya hasira ya Mungu kana kwamba ilikuwa kama moto. "Mungu pia amemwaga moto wa hasira dhidi yangu mimi" au" Mungu pia amenikasirikia mimi"

yeye ananihesabu mimi kama mmoja wa adui zake.

"yeye anafikiri juu yangu mimi kama adui yake"

Majeshi yake huja juu pamoja;

Ayubu anazungumza juu ya Mungu kumshambulia yeye kana kwamba Ayubu alikuwa mji na Mungu alikuwa anatuma jeshi kushambulia. "Mungu anatuma jeshi lake kunishambulia mimi"

kuniteka nyara kwa kundi kubwa kupigana na mimi

Mungu anazungumza juu ya Mungu kumshambulia yeye kana kwamba Ayubu alikuwa kama ukuta wa mji na jeshi la Mungu lilikuwa likiuangusha vibaya ukuta na kuuteka mji. "wanajeshi walikuwa wakiuharibu vibaya ukuta ili kupanda juu ya ukuta"

wakizunguka hema yangu.

Mungu anazungumza juu ya Mungu kumshambulia yeye kana kwamba Ayubu alikuwa hema yake na jeshi la Mungu likipiga kambi kumzunguka yeye na kujiandaa kumshambulia yeye. "wanapiga kambi kuzunguka hema yangu na kujiandaa kunishambulia mimi"

Job 19:13

Habari za Jumla:

Ayuba anaendelea kuzungumza kwa rafiki zake watatu.

Yeye amewaweka ndugu zangu mbali kutoka kwangu mimi;

kuwa mbali "mbali kutoka" kwa mtu fulani inawakilisha kutokutaka kuhusiana na yeye au kumsaidia yeye" Mungu amewasababisha ndugu zangu kukaa mbali na mimi" au " Mungu kuwasababisha ndugu zangu kukataaa kunisaidia mimi"

watu wangu wa karibu wote wamejitenga kutoka kwangu mimi

wasaidizi wangu wamejitenga wao wenyewe kuto kwangu" au " rafiki zangu hunitendea mimi kama mgeni"

Vizazi vyangu vimeniangusha mimi

"ndugu zangu mimi wameniacha bila msaada"

rafiki zangu wa karibu

"rafiki zangu wa karibu"

wamenisahamu mimi

Hii ina maana kwamba wao wamekataa kumtenda yeye kulingana na jinsi yeye na wao wamekuwa wakihusiana kwa kila mmoja wakati uliopita. Inamaanisha kwamba wao wanamtelekeza yeye. "wamenitelekeza mimi" au"kunipuuza mimi"

Job 19:15

habari za Jumla:

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa rafiki zake watatu.

hunihesabu mimi

"kunifikiria mimi"

Mimi nimekuwa mgeni katika macho yao

Kuona kwao kunawakilisha mtzazamo wao dhidi yake. "wao wanafikiri juu yangu mimi kama mgeni"

lakini yeye hanipi jibu

Jibu ni mwitiko wa kuita kwa Ayubu. "lakini yeye hajibu kwangu mimi" au " lakini yeye haji kwangu mimi"

japokuwa Mimi nimemsihi yeye kwa midomo yangu.

Tungo"kwa midomo yangu" inamaanisha Ayubu anazungumza" ingawa Mimi ninazungumza kwake yeye na kumwomba yeye."

Job 19:17

habari za Jumla:

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa rafiki zake watatu.

Pumzi yangu mimi ni chukizo kwa mke wangu;

Katika sentensi hii neno "pumzi" linawakilisha harufu ya pumzi yake yeye. Kama mtu fulani analaumika kwa mtu mwingine, ina maanisha kwamba yeye anaichukia. "Mke wangu anaichukia harufu ya kinywa changu"

wale ambao walizaliwa kutoka katika tumbo la mama yangu mimi.

Ayubu anamaanisha kaka zake na dada zake kwa njia hii kuonyesha kwamba wao ni watu ambao wanapaswa kumpenda yeye."kaka zangu mimi mwenyewe" au"kaka zangu na dada zangu"

wananichukia mimi;

"kunichukia mimi" au kunitenga mimi"

huzungumza dhidi yangu mimi.

"wao wananikejeli mimi" au" wananicheka mimi"

Rafiki zangu wote

"rafiki zangu wote wa karibu" au"rafiki zangu wote ambao huwaambia mambo yangu ya siri"

huzungumza dhidi yangu mimi

"wamenichukia mimi"

wamegeuka kinyume na mimi.

"wamenisaliti mimi"

Job 19:20

habari za Jumla:

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa rafiki zake watatu.

Mifupa yangu inashikamana kwenye ngozi yangu na kwenye mwili wangu;

Ayubu anazungumza juu ya mifupa yake, ngozi na nyama yake kuelezea mwonekano wake.Yeye alikuwa amekonda sana, na watu wangeweza kuona kwa urahisi mifupa yake yeye ilivyo. Lungha zingine zina nahau katika hili. " "Mimi sasa ni ngozi na mifupa" au " ngozi yake inashikamana na mifupa yangu"

Mimi ninaishi tu kwa ngozi ya meno yangu.

Hii nahau inamaanisha kwamba yeye anaishi kwa bahati tu, kuwa yeye karibia haishi."Mimi ninaishi kwa shida"

Iweni na huruma juu yangu mimi,

"muwe na huruma juu yangu"

kwa maana mkono wa Mungu umenigusa mim

Katika sentensi hii neno"alinigusa mimi" ni kiwakilishi cha neno "nipige mimi" Hii ni tashbiha kwa kufanya vitu ambavyo vinasabisha Ayubu ateseke. "kwa sababu Mungu amenitesa mimi"

Kwa nini mnanitesa mimi?

Ayubu anatumia swali hili kulalamika kuhusu jinsi rafiki zake wanavyomtendea yeye. "usinitese mimi....Mungu!"

kwa nini hamjatosheka bado kwa kula mwili wangu?

Ayubu anatumia swali hili kulalamika kuhusu jinsi rafiki zake wanavyomtendea yeye. Ninyi meumeza mwili wangu vya kutosha!" au "Acheni kuumeza mwili wangu mimi"

kwa nini hamjatosheka bado kwa kula mwili wangu?

Ayubu anazungumza juu ya rafiki zake wanaozungumza kwa ukatili kwake yeye kama vile walikuwa wanyama wakali wa porini wanakula wanyama wenzao. "Acheni kunishambulia mimi kwa maneno"

Job 19:23

Habari za Jumla"

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa rafiki zake watatu.

Laiti, hayo maneno yangu yangekuwa yameandikwa chini!

Mshangao huu unaeleza kile ambacho Ayubu anatamani kwa ajili yake."Mimi ninatamani kuwa mtu fulani angeyaandika chini maneno yangu"

maneno yangu

Tungo hii inawakilisha kile ambacho Ayubu anasema. "kile ambacho mimi ninakisema"

Laiti, hayo yangekuwa yameandikwa katika kitabu!

Mshangao huu unaeleza kile ambacho Ayubu anatamani kwa ajili yake."Mimi ninatamani kuwa mtu fulani angeyaandika katika kitabu"

Laiti, kwa kalamu ya chuma na risasi hayo yangekuwa yamechorwa katika mwamba siku zote!

Mshangao huu unaeleza kile ambacho Ayubu anatamani kwa ajili yake. "Mimi ninatamani kuwa mtu fulani angetumia kalamu ya chuma na risasi na kuyatunza katika pango siku zote"

kalamu ya chuma

Hiki kilikuwa kitendea kazi kilichotumika kuandika. kilikuwa kimetengenezwa kwa chuma ya kwamba watu waweze kuyaficha maneno katika mwamba"ni kifaa cha chuma"

risasi

Risasi ni madini laini ya chuma.Hatufahamu jinsi watu walivyotumia risasi wanapouchonga mwamba.Wanaweza kuwa wameijaza barua ya maandishi kwa risasi ili kuyafanya maandishi yadumu siku nyingi.

Job 19:25

Habari za Jumla:

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa rafiki zake watatu.

mkombozi wangu

Katika sentensi hii neno"mkombozi" linamaanisha mtu ambaye atamwokoa Ayubu kwa kthibitisha kuwwa Ayubu hana hatia., kurudisha heshima yake, na kumpa yeye haki. "Mtetezi wangu"

hata mwisho atasimama katika nchi;

Sentensi hii inamaanisha kusimama katika mahakama. Mkombozi atakuwa wa mwisho kuzungumza katika mahakama. "Yeye atahukumu ikiwa mimi ni mwenye hatia au hapana"mwisho atanitetea mimi katika mahakama"

baada ya ngozi yangu, hivyo ndivyo, mwili huu, unaharibiwa,

mwili wake yeye kuwa umeharibiwa au mwili wak kuoza baada ya yeye kuwa amekufa.

katika mwili wangu mimi Nitamwona Mungu.

Nyama yake inawakilisha mwili wake , na "katika nyama yangu" inamaanisha katika kuwa hai. Waakati Mimi ninaishi katika mwili wangu, Mimi nitamwona Mungu"

macho yangu mwenyewe-Mimi, na siyo mtu mwingine....nitamwona yeye

Neno"macho yangu"yanawakilisha Ayubu. Na tungo "macho yangu" "na" na "siyo mtu mwingie" kusisitiza kuwa Ayubu kwa hakika atamwona Mungu. Na siyo mtu mwingine atamwona Mungu na kumwambia Ayubu kuhusu yeye.

Figo zangu hushindwa ndani yangu

Watu walifikiri kwamba kwenye figo ndipo palipo na hisia. Hivyo figo kushindwa kufanya kazi inawakilisha yeye kuwa mwenye hisia nyingi sana. "Mimi ni mwenye hisia kali juu yake" au hisia zangu zinanitaabisha mimi kama vile nifikirivyo juu yake"

Figo zangu hushindwa ndani yangu

Maana za za sentensi hii zaweza kuwa : Ayubu anajisikia mwenye matumaini sana, mwenye shukrani, na mwenye furaha au Ayubu anajisikia mwenye kuchoka sana kusubiri kumwona mkombozi wake.

Job 19:28

habari za Jumla:

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa rafiki zake.

Kwa jinsi gani tutamtesa yeye?

Huu ni mshangao! Kumaanisha kuwaa wao kwa hakika watamtesa Ayubu au watamtesa yeye vikali sana.

Mzizi wa mahangaiko yake unakaa katika yeye;

"Mzizi" unawakilisha chanzo. "Yeye ni chanzo cha mahangaiko yake" au " Yeye amekuwa na matatizo haya yote kwa sababu ya kile ambacho yeye amekitenda"

ndipo uwe umeogopeshwa kwa ule upanga,

Sentensi hii ina maanisha hivi: Mungu anawahukumu wao, au Mungu anawaua wao. "kisha uwe na hofu kwamba Mungu anawaua", au "kisha uogope kwamba Mungu atakuua wewe"

kwa sababu ghadhabu huleta hukumu ya upanga,

Katika sentensi hii maneno "huleta" ni tashbiha kwa neno "matokeo" au "chanzo" Majina dhahania "ghadhabu" na "hukumu" yaweza kuelezwa na kivumishi "kasirika" na kitenzi "adhibu." Maana zaweza kuwa hizi: Hasira ya Mungu inaleta hukumu. "kwa sababu Mungu atakukasirikia wewe na kukuadhibu wewe" au " hasira ya rafiki za Ayubu inaleta hukumu. "kama mna hasira sana na mimi, Mungu atawaadhibu ninyi"

kuna hukumu."

Jina dhahania "hukumu" laweza kuelezwa na kitenzi "hukumu""Mungu huwahukumu watu"

Job 20

Job 20:1

habari za Jumla:

Sofari anamjibu Ayubu.

Sofari, Mnaamathi

Sofari wa mkoa wa Naamathi

Mawazo yangu yananifanya mimi nijibu kwa haraka

Mawazo ya Sofari kumfanya yeye kutenda jambo ina maanisha shauku yake kubwa kutenda jambo. "Mimi nahitaji sana kukujibu wewe haraka"

kwa sababu ya mashaka yaliyomo ndani yangu mimi.

Jina dhahania "hofu" laweza kuelezwa pamoja na kivumishi "kuhofu"Sababu ya hofu hii yaweza kuelezwa "Kwa sababu mimi naogopeshwa sana na wewe" au "kwa sababu nimeogopeshwa sana na kile ambacho umesema"

Mimi ninasikia kukemewa ambako kunaniondolea heshima mimi

Jina dhahania "kemea" laweza kuelezwa pamoja na kitenzi "kemea." "Mimi ninasikia wewe unanikemea mimi, na kile unachokisema kinaniondolea heshima mimi" au "wewe wanidhalilisha mimi kwa jinsi ambavyo unanikemea mimi"

roho kutoka katika ufahamu wangu hunijibu mimi.

katika sentensi hii "roho" inamaanisha fikra au wazo" wazo kutoka katika ufahamu wangu linanijibu mimi"

roho kutoka katika ufahamu wangu hunijibu mimi.

"roho" au wazo imesemwa kama vile ilikuwa mtu ambayo inaweza kumjibu Sofari. "Mimi nina wazo kutoka katika ufahamu wangu na sasa Mimi ninafahamu kile ambacho nilihitaji kufahamu"

roho kutoka katika ufahamu wangu hunijibu mimi.

yaliyomo katika jibu yanaweza kuelezwa kwa ufasaha. "wazo kutoka katika ufahamu wangu hunijibu mimi kuhusu namna nitakavyojibu kwako" au Mimi nina wazo kutoka katika ufahamu wangu , na sasa Mimi ninafahamu namna nitakavyokujibu wewe"

roho kutoka katika ufahamu wangu hunijibu mimi.

Kielezi cha jina "roho"chaweza kuelezwa pamoja na kitenzi "fikiri" na "fahamu" Kwa sababu ninavifahamu vitu, Mimi nimefikiri, na sasa Mimi ninafahamu jinsi nitakavyokujibu wewe.

Job 20:4

Habari za Jumla:

Sofari anaendelea kuzungumza na Ayubu.

Je, unafahamu kwamba ukweli huu kutoka enzi za kale kwa kitambo?

Sofari anatumia swali hili kumfanya Ayubu afikiri kwa kina kwa kile ambacho sasa atazungumza. "Hakika wewe unafahamu kile ambacho kimekuwa cha kweli tangu siku za mababu....kwa kitambo"

ushindi wa mtu mwovu ni mfupi,

jina dhahania"mshindi" laweza kuelezwa pamoja na vitenzi "ushindi" au "sherehekea." mtu mwovu hushinda kwa muda mfupi tu" au " mtu mwovu husherehekea kwa muda kidogo tu"

na furaha ya mtu asiyemcha Mungu hudumu kwa kitambo tu?

jina dhahania "furaha" laweza kuelezwa pamoja na kitenzi "furahia" au kivumishi "furaha"." Neno "kitambo" ni baragha kusisitiza kuwa muda ni mfupi sana ."mtu asiye mcha Mungu hufurahia kwa kitambo tu" au "mtu asiye mcha Mungu ana furahi kwa muda mfupi sana"

Job 20:6

Habari za Jumla:

Sofari anaendelea kuzungumza na Ayubu

Ingawa urefu wake

""Ingawa urefu wa mtu mwovu"

Ingawa urefu wake yeye hufikia juu kwenye mbingu,

Kielezi cha jina "urefu" chaweza kuelezwa pamoja na kivumishi "refu". Ingawa yeye ni mrefu kama mbingu"

Ingawa urefu wake yeye hufikia juu kwenye mbingu,

Urefu wa mtu mwovu unawakilisha heshima yake, au kiburi chake."Ingawa heshima yake inafika mpaka mbinguni" au "Ingawa kiburi chake kinafika mbinguni"

Ingawa urefu wake yeye hufikia juu kwenye mbingu,

katika sentensi hii "kufika mbinguni" kunawakilisha kuwa mkubwa sana "Ingawa heshima yake yeye ni kubwa" au Ingawa kiburi chake ni kikubwa"

Ingawa urefu wake yeye hufikia juu kwenye mbingu,

Kielezi cha jina "urefu" kinawakilisha heshima yake yeye au kiburi. Mawazo yote haya yanaweza kuelezwa pamoja na aina nyingine ya tungo."Japkuwa watu hufikiri kuwa yeye ni mtu mkuu sana" au" Japokuwa yeye ni mkuu"

na kichwa chake yeye kufikia kwenye mawingu

"japokuwa kichwa chake ni kirefu kama mawingu" " Hii pia iinawakilisha heshima yake yeye au kiburi chake kwa kuwa mkuu. Hii inamaana kama ile ya mistari iliyotangulia.

atapotea siku zote kama mavi yake yeye mwenyewe;

Mavi huchanganikana na udongo na kupotea. Rejeo hili kuhusu mavi linaweza pia kumaanisha kuwa mtu mwovu hana thamani. "atapotea siku zote kama mavi yake, ambayo hupotea kabisa katika udongo.

atapotea siku zote kama mavi yake yeye mwenyewe;

"atapotea siku zote kama mavumbi ambayo upepo huyapeperusha mbali"

Job 20:8

Habari za Jumla:

Sofari anaendelea kuzungumza kwa Ayubu.

Yeye ata

"Mtu mwovu ata"

atapaa mbali kama ndoto .... yeye atakuwa amefukuzwa mbali kama ono la usiku.

Katika sentensi hii neno "paa mbali" na "kufukuzwa mbali" yanawakilisha kutoonekana au kusahauliwa, kwa maana ndoto na maono hupotea wakati watu wanapozisahau. "Yeye hataonekana kama ndoto ....yeye atasahaulik akama ono la usiku"

na hataonekana tena

"na hakuna mtu yeyote atayemuona"

Jicho ambalo lilimuona yeye

Macho yanawakilisha mtu. "Mtu yeyote ambaye amemuona yeye", au "Watu waliomuona yeye"

mahali pake

Tungo "mahali pake yeye" inawakilisha wale walioishi katika sehemu yake yeye" "watu ambao huishi katika sehemu yake yeye' au" familia yake"

Job 20:10

Habari za Jumla:

Sofari anaendelea kuzungumza kwa Ayubu.

Watoto wake

"Watoto wa mtu mwovu"

mikono yake itaweza kurudisha utajiri wake.

Katika sentensi hii "mikono"inamaanisha watoto wa mtu mpumbavu. Wakati atakapokufa watoto wake watapaswa kurudisha kila kitu ambacho yeye alikichukua kwa watu wengine.

Mifupa yake imejaa nguvu za ujanani,

"Mifupa" yake inawakilisha mwili wake. Kuwa "umejawa" na nguvu za ujanani kunawakilisha kuwa na nguvu kama mtu kijana."Mwili wake una nguvu kama mwili wa mtu kijana"

lakini zitalala naye chini katika mavumbi.

Sentensi hii inamaanisha nguvu zake za ujanani "kulala chini katika mavumbi" kunawakilisha kupotelea mbali. " lakini nguvu zake za ujanani zitakufa maoja naye" au "lakini nguvu zake za ujanani hazitaonekana wakati atakapokufa"

Job 20:12

habari za Jumla:

Sofari anaendelea kuzungumza na Ayubu.

japokuwa uovu ni mtamu katika mdomo wake

Katika sentensi hii "uovu ni mtamu" tungo hii inawakilisha mtu ambaye anafurahia kufanya vitu. "Japokuwa kufanya vitu viovu inafurahisha, kama kuonja chakula kitamu katika mdomo"

japokuwa yeye anauficha yeye... hauruhusu kwenda

Tungo hii inawakilisha kutaka kuendelea kufurahia uovu kama vile mtu atakavyo kuendelea kuonja chakula kwa kukitunza katika mdomo.

chakula katika koromeo lake yeye hugeuka kuwa uchungu;

Wakati chakula kinapogeuka kuwa uchungu katika tumbo, inasababisha maumivu na ladha chungu. Hii ni tashbiha kwa mtu anayepitia mateso ya kufanya vitu viovu. Vito hivyo viovu, huwa kama chakula ambacho kimegeuka uchungu katika tumbo." au" cha maumivu kama chakula kilichogeuka kuwa kichungu ndani ya tumbo.

hugeuka kuwa sumu ya majoka ndani yake yeye.

Hii picha ni mbaya kuliko hata chakula chenye uchungu katika tumbo. Hii ni tashbiha inayoonyesha mtu akipitia mateso makali kwa kutenda vitu viovu. Madhara ya kufanya vitu viovu ni makali kama sumu ya majoka ndani yake"

majoka

"ni nyoka wenye sumu kali"

Job 20:15

Habari za Jumla:

Sofari anaendelea kuzungumza kwa Ayubu.

Yeye humeza chini utajiri, lakini yeye atautapika tena; Mungu atautoa nje kutoka katika tumbo lake

Sofari anazungumza juu ya kupata au kupoteza utajiri kana kwamba kilikuwa chakula ambacho mtu hula na kukitapika. "Mtu mwovu huwa mwenye mali nyingi lakini hpoteza utajiri wake kama mtu ambaye hukitapika chakula chake yeye. Mungu anamfanya kupoteza vyote"

Yeye humeza chini utajiri,

Maana zaweza kuwa hizi: kujikusanyia utajiri na kuunza kwa ubinafsi. "Mtu mwovu hupata hupata mali nyingi na huutuza wote kwa ajili yake yeyey mwenyewe" au" kujikusanyia mali katika njia za uovu""Mtu mwovu huiba mali nyingi"

Mungu atautoa nje kutoka katika tumbo lake yeye.

Katika sentensi hii: tungo: "kuutapika nje ya tumbo lake" ni ishara ya kumsababisha kuvitapika. Hii ni tashbiha inayoelezea kumsababisha mtu kupoteza utajiri wake.

toa

"tupa"

yeye atamumunya sumu ya majoka;

"kumumunya sumu ya majoka" kunawakilisha kufanya vitu viovu. Vyote ni hatari sana. Kufanya vitu viovu ni kuhatarisha maisha yake kama mtu anayemumunya sumu ya majoka"

majoka;

"nyoka wenye sumu kali"

ulimi wa nyoka mwenye sumu utamwua yeye.

Swira ni nyoka mwenye sumu kali . Ulimi wake unawakilisha mnga'to wake wenye sumu. Mng'ato wa Swira mwenye sumu unawakilisha mnga'to wake wenye sumu."Mng'ato wa Swira mwenye sumu utamwua yeye" au"Swira atamuuma yeye na yeye atakufa"

ulimi wa nyoka mwenye sumu utamwua yeye.

Swira anawakilisha uovu wa mtu. "uovu wake utamwua yeye kama kung'atwa na Swira.

Job 20:17

Hbari za J umla:

Sofari anaendelea kuzungumza kwa Ayubu.

vijito vya maji, wingi wa asali na siagi.

Vijito vya maji na wingi wa asali ni tashbiha kuwakilisha wingi. Asali na siagi kuwakilisha vitu vizuri ambavyo Mungu huwapa watu. ""wingi wa vitu vizuri ambavyo Mungu huwapa watu"

matunda ya kazi yake

"matunda ya kazi yake" inamaanisha matokeo ya kazi yake.Katika hoja hii inamaanisha vitu ambavyo mtu mwovu ameiba."vitu ambavyo amefanya kazi kuvipata" au"vitu ambavyo ameviiba"

Job 20:20

Hakuna chochote kilichoachwa ambacho yeye hakukimeza;

"Yeye alimeza kila kitu, na hakuna kitu chochote kilichobakia" au"hakuna kitu chochote kilichobakia kwa sababu yeye amemeza kila kitu"

Hakuna chochote kilichoachwa ambacho yeye hakukimeza;

"kumeza"kunawakilisha kuchukua vitu kwa ajili yake mwenyewe. "Hakuna chochote ambacho hakukichukuwa kwa ajili yake mwenyewe" au" Yeye alichukua kila kitu kwa ajili yake mwenyewe, na hakuna kitu chochote kilichobakia"

yeye ataanguka katika mahangaiko

"ghafla yeye atapittia mahangaiko"

mkono wa kila mmoja ambaye yuko katika umaskini utakuja kinyume chake yeye.

katika sentensi hii "mkono" unawakilisha nguvu, na "mkono... utakuja dhidi yake" unawakilisha watu kumshambulia yeye. Kielezi cha tendo "umaskini"chaweza kuelezwa pamoja na kivumishi "maskini" "kila mtu aliye katika umaskini atamshambulia yeye" au "kila mtu ambaye ni maskini atamshambulia yeye"

Job 20:23

Habari za Jumla:

Sofari anaendelea kuzungumza kwa Ayubu.

kulijaza tumbo lake

"kulijaza tumbo lake" inamaanisha kula sana.

Mungu atatupa hasira ya ghadhabu yake juu yake yeye

"katika hasira ya ghadhabu yake" ina maanisha hasira ya Mungu na adhabu yake.Kutupa adhabu juu yake ni kumwadhibu yeye vikali sna. "Mungu atakuwa mwenye hasira na kutupa chini adhabu yake juu yake"au"Mungu atakasirika na kumwadhibu yeye vikali sana"

Mungu ataunyeshea chini juu yake yeye

"Mungu ataisababisha inyeshe chini juu yake." "kunyesha chini juu yake" inawakilisha kusababisha adhabu nyingi kutokea kwa mtu. "Mungu atamwadhibu yeye vikali"

atakimbia kutoka katika silaha ya chuma,

Silaha ya chuma inawakilisha mtu kuibeba yenyewe. "atakimbia kutoka kwa mtu anayebeba silaha ya chuma"

upinde wa shaba utampiga yeye

Upinde unawakilisha mtu anayepiga upinde kwa kutumia upinde. "Mtu mwenye upinde wa shaba atampiga yeye"

ini

Hii ni sehemu yenye muhimu wake mkubwa katika mwili. Ikiwa mtu atapiga upinde kwenye ini, mtu aliyepigwa atakufa.

watesi huja tena juu yake.

Maneno haya yanamwakilisha yeye kwa ghafla anakuwa amefadhaishwa"

Job 20:26

Giza lililo kamilika limetunzwa kwa akiba zake;

"Giza lililokamailika" ni tashbiha kuonyesha uharibifu. "Uharibifu umetunzwa kwa ajili ya akiba zake yeye"au"Akiba zake yeye mwenyewe zitaharibiwa"

moto usiopulizwa utamla yeye

katika tungo hii neno "kumeza" ni tashbiha inayomaanisha kuharibu."mto ambao haukupulizwa utamharibu yeye"

moto usiopulizwa utamla yeye

Tungo "haukupulizwa" inamaanisha kuwa kuwa hakuna mwanadamu ambaye atauwasha moto. Ni Mungu atauleta moto. "moto ambao haukuwashwa na mwanadamu utamharibu yeye"au" Mungu atauleta moto kumharibu yeye"

utameza

Neno hili lemetafsiriwa hivi: "kumeza" ni tashbiha kumaanisha kuharibu."mto utaharibu"

Mbingu...na nchi

Tungo hii inaweza kutafsiriwa hivi: Wale anaoishi katika mbingu na juu ya nchi, au Sofari anazielezea mbingu na nchi kana kwamba ni binadamu ambaye atashuhudia katika mahakama dhidi ya mtu mwovu.

Job 20:28

Habari za Jumla:

Sehemu hii ni hitimisho la hotuba ya Sofari kwa Ayubu.

toweka

"kutoonekana" au "enda mbali"

bidhaa zake zitamwagika mbali

Maneno "mwagika mbali" yanawakilisha kuondolewa mbali kutoka kwake."bidhaa zake zitachukuliwa mbali kutoka kwake, kama bidhaa zinazoelea katika mafuriko"

siku ya ghadhabu ya Mungu.

Neno "ghadhabu" linawakilisha kuadhibiwa. Kielezi cha jna "ghadhabu" chaweza kuelezwa pamoja na kitenzi "adhibu""siku ambayo Mungu huwadhibu watu"

Hii ndiyo sehemu ya mtu mwovu kutoka kwa Mungu,

Maneno "sehemu kutoka kwa Mungu" yanawakilisha kile ambacho Mungu amekikusudia kitokee kwa mtu fulani. Kimezungumzwa kana kwamba kilikuwa kitu ambacho Mungu angempa yeye. "Hiki ndicho ambacho Mungu amekikusudia kitokee kwa mtu mwovu"

urithi uliotunzwa akiba na Mungu kwa ajili yake yeye."

Tungo hii inawakilisha kile ambacho ameamua kinapaswa kitokee kwa mtu fulani. Kimezungumzwa kana kwamba kilikuwa kitu ambacho Mungu angempa yeye hapo kabla kama urithi. "Kile ambacho Mungu amekipanga kumpa yeye" au "kile ambacho Mungu amekikusudia lazima kitokee kwake"

Job 21

Job 21:1

Sentensi unganishi

Ayubu anaanza kujibu mashitaka ya Sofari

Univumilie

"Uniruhusu" au " uwe mstahimilivu kwangu"

Endelea kunidhihaki

" unaweza kuendelea kunidhihaki"

Job 21:4

Sentensi Unganishi.

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa rafiki zake.

Je mimi, malalamiko yangu ni dhidi ya mtu? Kwa nini nisiwe mvumilivu?

Ayubu anatumia maswali kusisitiza kuwa ni hali ya kawaida kwake kumlalamikia Mungu.KT: "Simlalamikii mtu . ninahaki ya kutokuwa na uvumilivu"

weka mkono wako juu ya kinywa chako

"funika kinywa chako kwa mkono wako" Maneno haya yanaweza kumaanisha kwamba 1) huu ni mwitikio wa kuwa katika mshangao. KT: " funika kinywa chako kwa mkono wako" au 2) hiki ni kiashiria kuwa mtu hataongea . KT: "usiseme lolote"

mashaka yameushika mwili wangu

" hofu inasababisha mwili wangu kutetemeka" au "ninatetemeka kwa hofu"

Job 21:7

Sentensi unganishi

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa rafiki zake.

Kwa nini watu waovu wanaendelea kuishi na kuwa wazee na kustawi katika nguvu nyingi?

Ayabu anatumia swali hili kuonesha kuwa rafiki zake walikosea kudhani kwamba watu waovu mara nyingi hupatwa na mateso. KN: " watu waovu huendelea kuishi, huzeeka, na kuwa na utajiri zaidi"

Wazao wao huimarika pamoja nao katika upeo wao...kizazi chao mbele ya macho yao.

Vishazi hivi viwili vinamaana ya jambo moja na vinaweka msisitizo kuwa jambo hili ni la kweli.

katika upeo wao... mbele ya macho yao

Misemo hii inamaanisha jambo moja kwa sababu "macho" yanahusiana na upeo wa kuona. Watu waovu huwaona wazoa wao wakistawi na kutajirika.

Nyumba zao

Hapa "nyumba" inamaanisha wanafamilia wanaoishi humo. KT: "Familia zao"

fimbo ya Mungu

inamaanisha adhabu ya Mungu.

Job 21:10

Sentensi unganishi

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa rafiki zake.

hapotezi ndama wake mchanga

" haharibu mimba" au " ndama wake huzaliwa mathubuti na mwenye afya"

watoto wao kama kundi

Ayubu anawalinganisha watoto hawa na wanakondoo ili kusisistiza kwamba hukimbia, hucheza, na wanafuraha.

tari

ni chombo cha muziki chenye ngoma inayoweza kupigwa pamoja na vipande vya chuma pembeni ambavyo hutoa sauti wakati chombo hicho kinapotikiswa.

Job 21:13

Sentensi unganishi

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa rafiki zake.

siku zao

"muda wao wa kuishi"

Hushuka taratibu kwenda kuzimu

KT: "hufa kwa amani"

njia zako

inamaanisha jinsi Mungu anavotaka watu waenende.

Mwenyezi ni kitu gani, hata itupase kumwabudu? Ni faida gani tungepata kama tungemwomba?

watu waovu hutumia maswali haya katika kumdhihaki Mungu. KT: Hatuamini kwamba huyu Mungu Mwenyezi anastahili tumwabudu. Hawezi kufanya chochote kwa ajili yetu"

Job 21:16

Sentensi unganishi

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa rafiki zake.

Tazama, je kufanikwa kwao hakupo mikono mwao mwenyewe?

hapa "mikono" inamaanisha nguvu zao au utawala wao. Ayubu anatumia swali hili kutoa changamoto kwa rafiki zake. KT: "Tazama, watu hawa waovu wanasema kwamba wamesababisha mafaniki wao wenyewe!"

Je ni mara ngapi... msiba wao huwajilia?

Ayubu anatumia swali hili kusisitiza kuwa yeye anaona kwamba Mungu hawaadhibu waovu mara nyingi. KT: "si mara nyingi ... msiba wao huwapata "

taa ya watu waovu imezimwa

Ayubu analinganisha kuzima taa na kufa. KTN: "Mungu husababisha wafe ghafla"

Ni mara ngapi hutokea... katika hasira yake?

Ayubu anatumia swali hili la pili kuweka mkazo kuwa inaonekana mara nyingi Mungu huwa hawaadhibu waovu. KTN: "Si mara nyingi ... katika hasira yake."

Ni mara ngapi ... dhoruba huwabeba?

Ayubu anatumia swali hili la tatu kuweka mkazo kuwa inaonekana mara nyingi Mungu huwa hawaadhibu waovu.KTN: "Si mara nyingi ... dhoruba huwabeba."

wanakuwa kama mabua mbele ya upepo au kama makapi ambayo huchukuliwa na dhoruba

Kifo cha waovu kinaongelewa kana kwamba ni makapi yasiyofaa na mabua yapeperushwayo.KTN: "Mungu huwaondoa kama upepo upeperushao makapi"

Job 21:19

Sentensi Unganishi

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa rafiki zake.

Ninyi mwasema

maneno haya yanaonesha kuwa Ayubu anawanukuu rafiki zake.

Mungu huweka hatia ya mtu kwa ajili ya watoto wake kuilipa

Hatia inaongelewa kama kitu ambacho kinaweza kuhifadhiwa kwa matumizi ya baadaye. Hapa kulipa inamaanisha adhabu kwa ajili ya dhambi. KTN: "Mungu hutunza kumbukumbu ya dhambi za mtu, kisha huwaadhibu watoto wa mtu huyo kwa matendo yake maovu"

alipe yeye mwenyewe

Ayubu anaanza kutoa mawazo yake. KTN: " Lakini mimi nasema, alipe yeye mwenyewe"

Macho yake mwenyewe yaone

"Macho" ni rejea kwa mtu.KTN: "aweze kuona yeye mwenyewe"

anywe ghadhabu Mwenyezi

Ghadhabu ya Mungu inasema kana kwamba ni kinywaji ambacho mtu anaweza kuonja. Ayubu anataka waovu wapate adhabu ya Mungu.

Kwani anajali nini kuhusu familia yake baada ya idadi ya miezi yake kuondolewa?

Ayubu anatumia swali kuonesha kuwa kuwaadhibu watoto wa mtu mwovu haina nguvu.KTN: "Kwani mtu mwovu hajali kuhusu familia yake baada ya kufa!"

idadi ya miezi yake kuondolewa

hii ni namna ya staha kusema anapofariki.

idadi ya miezi yake

Hii inarejea urefu wa miaka ya maisha yake.

Job 21:22

Sentensi Unganishi

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa rafiki zake.

Mtu yeyote anaweza kumfundisha Mungu maarifa ikiwa yeye huwahukumu hata wale walio wakuu?

Ayubu anauliza swali kusisitiza kwamba Mungu anajua kila kitu. KTN: "Ni wazi, hakuna mtu anayeweza kumfundisha Mungu chochote kwani yeye huwahukumu hata wale walioko mbinguni."

walio wakuu

inaweza kumaanisha kuwa 1) "wale walioko mbinguni" au 2) "watu mashuhuri"

mtu mmoja hufa katika nguvu zake kamili.

Ayubu anamlinganisha mtu huyu afaye katika afya na amani na mtu afaye katika hudhuni na maumivu. KTN: "Kama kuma watu wawili, mmoja anaweza kufa katika nguvu zake kamili"

mwili wake umejaa maziwa

hii inamaana kwamba mtu yupo katika afya njema.

mwili wake umejaa maziwa... uboho wa mifupa yake umarainishwa na katika afya nzuri.

hii inamaana kwamba mtu yupo katika afya njema.

mwili wake umejaa maziwa

Neno "maziwa" linamaana ya "mnene" KTN: "mwili wake umejaa mafuta"

uboho wa mifupa yake umarainishwa na katika afya nzuri.

hii ni nahau ikimaanisha kuwa mwili wake una ujana na afya njema.

Job 21:25

Sentensi Unganishi

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa rafiki zake.

mtu mwingine hufa

Ayubu anamlinganisha mtu huyu na mtu ambaye hufa katika amani 21:22

katika uchungu wa roho

"Roho" inamaanisha mwanadamu kamili. KTN: 'kwa uchungu na majuto" au " baada ya kuishi maisha ya huzuni"

pasipo kuonja mema yoyote

KTN:"akiwa ameonja vitu vibaya tu"

Hao vilevile hulala chini katika mavumbi

Hii ni kusema kwa staha kuwa hao hufa. KTN: " Hao wote hufa na watu huwazika"

Minyoo huwafunika wote

minyoo huhusiana na kuoza kwa mizoga. KTN "katika uchafu minyoo hula mizoga ya miili yao"

Job 21:27

Sentensi unganishi

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa rafiki zake.

Tazama

Ayubu anatumia neno hili kuleta usikivu kwenye maneno yanayofuata. KTN: " angalia "

Sasa nyumba ya mfalme ipo wapi? ipo wapi hema ambapo mtu mwovu aliishi hapo mwanzo?

Maswali yote hay yana maanisha jambo moja. KTN: "Tazama, nyumba ya mtawala mwovu haipo. Hema ya mtu mwovu imetoweka"

Job 21:29

Setensi Unganishi

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa rafiki zake.

Je hamjawaliza watu wasafirio? Je hamjui viashiria wavyoweza kuwaambia ... kwa siku ya ghadhabu?

Ayubu anawakemea rafiki zake kwa kutumia maswali haya kuwa hawajajifunza kwa watu wasafirio. KTN: "Ninyi mnapaswa kuwasikiliza wale waliosafiri hadi sehemu za mbali. watawaambia ... kwa siku ya ghadhabu."

mtu mwovu huindwa kwa siku ya msiba ... huongozwa kwa siku ya ghadhabu

virai hivi vina maana sawa: KTN: "Mungu humhifadhi mtu mwovu wakati anapoleta maafa"

Job 21:31

Sentensi Unganishi

Ayubu anaendelea kuzungumza kwa rafiki zake.

Ni nani ataishutumu njia ya mtu mwovu kwenye uso wake?

Ayubu anatumia swali hili kupinga dhana ya kuwa waovu mara zote hupatwa na hukumu. KTN: ' Hakuna anayemshutumu mtu mwovu kwenye uso wake"

kwenye uso wake

Hapa inamaana kuwa hakuna mtu atakaye kwenda moja kwa moja kwake na kumshutumu.

Ni nani atamlipiza kwa yale aliyotenda?

Ayubu anatumia swali hili kupinga imani ya rafiki zake kuwa waovu mara zote hupatwa na hukumu. KTN: ' Hakuna mtu anayemlipiza mwovu kwa mambo mabaya aliyotenda"

atazikwa

KTN: " Watu watambeba"

Madonge ya bondeni yatakuwa matamu kwake

Maana yake ni kwamba mtu mwovu atakuwa na kifo chema na maziko mema baada ya kutimiza maisha yake. KTN: "atafurahia kufukiwa kwa uchafu wa bondeni" au " atafurahia kuzikwa katika uchafu wa bonde"

watu wote watamfuata, kutakuwa na watu wengi mbele yake

Ayubu anaweka makazo kuwa kundi kubwa la watu watakuwepo katika harakati za mazishi yake kutoa heshima. KTN: "idadi kubwa ya watu watakwenda kwenye eneo la makaburi; baadhi wakiwa mbele na wengine nyuma"

Job 21:34

Sentensi Unganishi

Hili ni hitimisho la mazungumzo ya Ayabu kwa rafiki zake.

imekuwa basi kunifariji kwa upuuzi, kwani katika majibu yenu hakuna kitu isipokuwa uongo?

Ayubu anatumia swali kuwakaripia rafiki zake. KTN: " haiwezekani mnifariji kwa upuuzi. majibu yenu yote ni uongo."

Job 22

Job 22:1

Elifazi Mtemani

Jina la mtu, angalia 2:11

Je mtu anaweza kumfaa Mungu? Je mtu mwenye busara anaweza kumfaa Yeye?

Elifazi anatumia maswali kuweka mkazo kuwa matendo ya mtu au hekima havina faida kwa Mungu. KTN: "Mtu hawezi kumfaa Mungu. Mtu mwenye busara hawezi kuwa na faida kwake faida kwa kwake"

Je kuna furaha yoyote kwa mwenyezi kama wewe ni mwenye haki? Je ni faida kwake kama utazifanya njia zako kuwa timilifu?

Sentensi zote zina maana moja. Elifazi anatumia maswali kukazia kuwa matendo yake Ayubu hayana msaada kwa Mungu.KTN: "Mwenyezi hapokei furaha yoyote kama wewe ni mwenye haki. Hafaidiki na chochote kama utazifanya njia zako kuwa timilifu"

Job 22:4

Sentensi Unganishi

Elifazi anaendelea kuongoa kwa Ayubu.

Je anakukemea na kukuhukumu kwa sababu ya kumcha yeye? Je uovu wako siyo mkuu? Je hapana mwisho wa maovu yako?

Elifazi anatumia maswali kumkaripia na kumlaumu Ayubu kwa kutenda dhambi za kutisha. KTN: "Ni kuwa kuwa hujajitoa kwake kikamilifu ndiyo maana Mungu anakukea na kukuhukumu! Hapana, kama ujuavyo, anakuhukunu kwa sababu uovu wako ni mkuu na unaendelea kutenda dhambi"

Job 22:6

Sentensi Unganishi

Elifazi anaendelea kuongoa kwa Ayubu.

Umedai dhamana ya mkopo

Maana yake mkopeshaji anachukua kitu kutoka kwa mkopaji ili kuhakikisha kwamba mkopaji atalipa.

umetwaa vazi kwa walio uchi

Elifazi anamshutumu Ayubu kuchukua nguo kutoka kwa watu masikini waliomkopa kama dhamana

ulimnyima mkate

hapa "mkate" unawakilisha chakula kwa ujumla

alimiliki nchi.. aliishi ndani yake

Elifazi anamshutumu Ayubu kuchukua eneo kutoka kwa watu masikini na wala hakuwaruhusu kuishi sehemu ile.

alimiliki nchi

"alimiliki eneo kubwa la ardhi"

Job 22:9

Sentensi Unganishi

Elifazi anaendelea kuongoa kwa Ayubu.

umewafukuza wajanae hali ya utupu

uliwafanya wajane waondoke bila kitu chochote

Wajane

wanawakea ambao waume zao wamefariki

mikono ya yatima imevunjika

hapa "mikono" inarejea nguvu. KTN: 'hata uliwakandamiza yatima"

mitego imekuzunguka ...kuna giza ..kwenye maji mengi.

sitiari zote hizi maana yake kuna shuda na hatari kumzunguka Ayubu kwa sababu ya dhambi zake.

kwenye maji mengi.

" kwenye mafuriko"

Job 22:12

Sentensi Unganishi

Elifazi anaendelea kuongoa kwa Ayubu.

Je Mungu hayupo kwenye kimo cha mbingu?

Elifazi anatumia swali hili kudokeza kwamba Mungu anaiona dhambi ya Ayubu na atamuhukumu. KTN: " Mungu yupo katika vimo vya mbingu na anaona kila kitu kinachotokea duniani"

tazama kimo kwenye kima cha nyota , je zipo juu kiasi gani!

Elifazi amaanisha kuwa Mungu yupo juu kuliko nyota. KTN: Angalia jinsi nyota zilivyo juu . Mungu yupo juu kuliko hizo nyota"

Je Mungu anajua nini? je anaweza kuhukumu kwenye mawingu mazito?

Elifazi anatumia maswali haya kumaanisha kwamba Ayabu amasema mambo haya dhudi ya Mungu. KTN: " Mungu hajui kitu gani kinatokea duniani. anakaa kwenye wingu la giza na hawezi kutuhukumu sisi."

yeye hutembea kwenye kuba ya mbingu

Kuba inarejea kwenye mpaka ambao watu wa kale waliamini ulitenganusha dunia na mbingu. KTN "anaishi mbali sana kwenye mbingu kuona ni nini kinatokea hapa"

Job 22:15

Sentensi Unganishi

Elifazi anaendelea kuongoa kwa Ayubu

utaendeza njia ya zamani ambayo walitembea watu waovu.

Kutenda matendo mabaya kunazungumziwa kama kutembea kwenye njia. KTN: " utaendelea kufanya mambo wafanyayo watu waovu"

wale ambao walinyakuliwa

"wale waliokufa" au wale ambao Mungu aliwaondoa"

wale ambao misingi yao imetoweshwa kama mto

kifo cha watu waovu kinaongeleawa kana kwamba ni majengo yaliyokuwa na misingi yake ambayo ilikwishwa haribiwa na mafuriko.

Mwenyezi anaweza kufanya nini

Elifazi ananukuu swali ambalo waovu hutumia kumdhihaki Mungu. KTN "Mwenyezi hawezi kufanya chochote kwetu!"

Job 22:18

Sentensi Unganishi

Elifazi anaendelea kuongoa kwa Ayubu

mipango ya waovu ipo mbali nami

"mbali nami" ni nahau ambayo inamaanisha kuwa Elifazi anawakana waovu. KTN: "lakini sitasikiliza mipango yao miovu"

huona maangamizi yao

"hujua kitakacho tokea kwa waovu"

huwcheka kwa dharau

"hudhihaki watu waovu"

wale walio inuka juu dhidi yetu wamekatiliwa mbali.

"walio inuka juu" inamaanisha watu waovu. KTN: "Mungu amewaharibu watu waovu waliotuumiza"

Job 22:21

Setensi Unganishi

Elifazi anaendelea kuongoa kwa Ayubu

Sasa

Elifazi anatumia neno sasa kutoa utangulizi wa jambo muhimu analotaka kusema.

maelekezo kutoka katika kinywa chake

"kutoka kwenye kinywa chake" inawakilisha yale ambayo Mungu amekwisha sema. KTN" "maelekezo ya ambayo Mungu a mekwisha kusema."

uyahifadhi maneno yake

KTN: "amri zake uziweke kuwa akiba"

moyo wako.

moyo unarejea mawazo ya Ayubu. KTN: "akili zako"

Job 22:23

Senensi unganishi

Elifazi anaendelea kuongoa kwa Ayubu

utajengwa

KTN: "atakuponya na kukufanikisha tena"

kama udhalimu utauweka mbali kutoka katika hema yako

picha ya udhalimu inaonyeshwa kana kwamba ni mtu anayeishi katika nyumba ya Ayubu ambaye anatakiwa kuondolewa. KTN: "ikiwa wewe na kila mtu katika nyumba yako mtakoma kutenda dhambi"

Hazina zako ziweke chini kwenye mavumbi

hazina kuiweka kwenye mavumbi ni kuitazama kama kitu ambacho hakina thamani.KTN: ufikirie utajiri wako kama ni kitu ambacho siyo cha muhimu kama vile mavumbi"

dhahabu ya ofiri miongo mwa mawe ya vijito.

kuiweka dhahabu katika mfereji ni kuiona kitu kisicho na thamani kama mawe. KTN: " dhahabu yako isiwe na thamani kama mawe kwenye kijito"

Ofiri

hili ni jina la ukanda maarufu kwa dhahabu yake.

Mwenyezi atakuwa hazina, fedha ya thamani kwako

hii inamaana Mungu atakuwa wa thamani zaidi kwa Ayubu kuliko hazina yoyote.

Job 22:26

Sentensi Unganishi

Elifazi anaendelea kuongoa kwa Ayubu

utainua uso wako kwa Mungu

Maana yake kwamba Ayubu hataona aibu tena bali atamwani Mungu. KTN: " utaweza kumkabili kwa ujasiri"

itathibitishwa kwako

KTN: "Mungu atakufanya ufanikiwe"

mwanga utang'aa juu ya njia zako

KTN: "itakuwa kama mwanga unaong'aa kwenye barabara mbele yako"

Job 22:29

Sentensi Unganishi

Elifazi anaendelea kuongoa kwa Ayubu

mwenye macho ya kujishusha

macho ya kujishusha inarejea unyenyekevu. KTN: ' mtu mnyenyekevu"

mtu ambaye hana hatia

hata mtu ambaye si mwungwana

utaokolewa kupitia usafi wa mikono yako

maana yake "Mungu atakuokoa kwa sababu ya usafi wa mikono yako"

kupitia usafi wa mikono yako

"usafi" inamaana ya kutokuwa na hatia "mikono" inamaana ya matendo afanyayo mtu. KTN: " kwa sababu unatenda yaliyo haki"

Job 23

Job 23:1

Hata leo malalamiko yangu ni mchungu

"Hata leo" ni msisistizo kuwa mabishano ya marafiki zake hawajabadili hali ya Ayubu kabisa. KTN: " pamoja na yote mliyosema, malalamiko yangu bado na uchungu"

mkono wangu ni mzito kwa sababu ya kuugua kwangu.

hii inaweza kumanisha kuwa1)" ninaweza kuinua mkono wangu kwa sababu ya kuugua kwangu" au 2) mkono wake unaendelea kuniteda pamoja na kuugua kwangu" neno mkono linarejea nguvu ya Mungu katika kuhukumu .

Job 23:3

Sentensi Unganishi

Ayubu anaendelea kuongea

Laiti, ningejua ambapo ... laiti, ningekuja

mistari hii miwili inamaana moja na inasisitiza hamu ya Ayubu kukutana na Mungu.

ningempata

" ningempata Mungu"

Ingeweka dawaa yangu ... kukijaza kinywa changu

mistari hii miwili inamaana moja na inasisitiza hamu ya Ayubu kueleza hali ya ke kwa Mungu.

kukijaza kinywa changu kwa hoja

KTN: "ningezungumza hoja za ngu zote"

Ningejifunza maneno ... ambacho angesema kwangu

mistari hii miwili inamaana moja na inasisitiza hamu ya Ayubu kusikia jibu la Mungu.

maneno ambayo angenijibu

"jibu ambalo angelinipa"

Job 23:6

Sentensi unganishi

Ayubu anaendelea kuongea

Je

"Mungu angelieweza"

Ambapo

inarejea sehemu ambapo Mungu yupo

je angeona kuwa sina hatia milele katika kuhukumu kwangu

KTN: "kuhukumu kwangu kungeliniweka huru daima" au "Mungu, ambaye ni hakimu wangu, angesema kuwa sina hatia kabisa"

Job 23:8

Sentensi Unganishi

Ayubu anaendelea kuongea

mashariki... magharibi .. kaskazini ... kusini

kwa kutaja pande hizi nne, Ayubu anasisitiza kwamba alitazama kila mahali.

Job 23:10

Sentensi Unganishi

Ayubu anaendelea kuongea

anaijua njia ninayoiendea

KTN: "Mungu anajua ninachofanya"

nitatoka kama dhahabu

Ayubu anaamini kuwa jaribio litamthibitisha kuwa mkamilifu kama dhahabu iliyosafishwa. KTN: "ataona kuwa nipo mkamilifu kama dhahabu ambayo uchafu wake wote umechomwa"

Mguu wangu umeshikamana kwenye hatua zake

"mguu wangu" inarejea kwa Ayubu. KTN: '"Nimeifuata njia aliyonionyesha"

nimeitunza njia yake

utii wa Ayubu unazungumziwa kama kutembea katika njia ambayo Mungu amemwelekeza" KTN: "Nimefanya alichoniambia"

sikungeukia upande

"fuata kwa usahihi"

sikurudi nyuma kutoka kwenye

KTN: "nimetii alichoamuru"

ya midomo yake

tungo hii inarejea ujumbe ambao Mungu alisema.. KTN: "ambacho alisema"

Nimeyatunza kwenye moyo wangu

hapa "moyo wangu"inarejea kwenye utu wa ndani wa Ayubu. KTN: "nimetunza katika utu wangu wa ndani" au "daima nafikiria juu yake"

maneno ya kinywa chake

hii inarejea kauli ya Mungu. KTN: "alichosema"

Job 23:13

Sentensi Unganishi

Ayubu anaendelea kuongea

Lakini yeye ni wa namna ya pekee, ni nani awezaye kumgeuza?

Ayubu anatumia swali hili kusisitiza kuwa Mungu ni wa pekee. KTN: "Lakini hakuna mwingine kama yeye, na hakuna wa kubadilisha nia yake." au "lakini yeye peke yake ni Mungu, na hakuna anayeweza kumshawishi"

Anachotaka, hukifanya

"anatimiza chochote anachotaka kufanya"

yeye huzitimiza amri zake dhidi yangu

" ananitendea ambacho alisema angefanya"

yapo mengi kama hayo

"anamipango yenye kufanana kwa ajili yangu"

Job 23:15

Sentensi Unganishi

Ayubu anaendelea kuongea

Maelezo ya Jumla

mistari hii kila mmoja upo katika muundo sambamba ili kusisitiza wazo kuu analotoa Ayubu.

maana Mungu ameufanya moyo wangu dhaifu; mwenyezi amenitaabisha

Hii mistari miwili inamaanisha jambo moja na inasisitiza kuwa Ayubu anamwogopa sana Mungu.

ameufanya moyo wangu dhaifu

mtu ambaye moyo wake ni dhaifu ni yule ambaye tishika au kujaa hofu.KTN " amenifanya niogope"

sikufikishwa mwisho kwa giza

inaweza kumaanisha 1) "giza nene mbele yangu halikufanya ninyamaze" au 2) "siyo giza lilonitupa nje" au "Mungu amenikatilia mbali, wala siyo giza"

Uso wangu

inamaanisha "mimi"

Job 24

Job 24:1

Sentensi Unganishi

Ayubu anaendelea kuongea

kwa nini nyakati za kuwahukumu watu waovu hazijapangawa na Mwenyezi?

Ayubu anatumia swali hili kuelezea fadhaa zake kuwa Mungu hajawahukumu waovu. KTN: " Sielewi kwa nini Mungu hajapanga muda ambapo atawahukumu watu waovu." au "Mwenyezi angapnga muda ambapo angewahukumu watu waovu"

Kwa nini wale ambao ni waaminifu kwa Mungu huona siku zake za hukumu zikija?

Ayubu anatumia swali hili kuelezea fadhaa zake kuwa wenye haki hawajamwona Mungu akihukumu uovu. KTN: "Inaonekana kuwa wale ambao humtii Mungu hawamwoni akiwahukumu waovu" au "Mungu angeonyesha siku ambapo atawahukumu waovu kwa wale wenye kumjua"

Job 24:2

Sentensi Unganishi

Ayubu anaendelea kuongea

alama za mipaka

haya ni mawe au vitu vingine kunyesha mpaka kati ya maeneo yanayomilikiwa na watu mbalimbali.

malisho

"konde la majani" au "viwanja vya kuchungia"

hutwaa

"wanaiba"

ambao hawana baba

"yatima" au "watoto ambao wazazi wao wamefariki"

huchua ng'ombe wa mjane kama rehani

"huchukua ng'ombe wa mjane ili kuwa hakikisho kwamba wajane watalipa pesa walizowakopesha

mjane

mwanamke ambaye amefiwa na mume wake.

dhamana

mwazimishaji alichukua kitu chochote kutoka mwazimaji ili kuhakikisha kuwa mwazimaji huyo atalipa.

nje ya njia yao

toka kwenye njia

watu masikini nchi waote hujificha

watu wengi masikini huwaogopa watu waovu.

Job 24:5

Sentensi Unganishi

Ayubu anaendelea kuongea

Watu hawa msikini huenda kwenye kazi zao mithili ya punda mwitu kwenye nyika, wakitafuta chakula kwa bidii

watu hawa ambao ni masikini wanaongelewa kana kwamba ni punda mwitu wasiojua ni wapi watapata chakula. KTN: "watu hawa masikini huenenda wakitafuta chakula kama vile punda mwitu kwenye nyika"

punda mwitu

"punda wasiomilikiwa na mtu au kuangaliwa"

watu masikini huvuana usiku ... wanakimulika zabibu.

hii mistari miwili inaeleza jambo moja na yote inasisitiza kwamba watu hawa wananjaa sana hivyo wanalazimika kuiba chadkula wakati wa usiku.

Hulala uchi ...hawana cha kujifunika

hii mistari miwili inaeleza jambo moja na yote inasisitiza kwamba watu hawa hawana mavazi ya kutosheleza kujisitili.

Job 24:8

Sentensi Unganishi

Ayubu anaendelea kuongea

wamelowana kwa manyunyu ya milimani

" wanlowana wakati inaponyesha milimani"

yatima kutoka kwenye maziwa ya mama zao

"maziwa" inarejea kwa mama. maana yake kuwa yatima hawa bado wadogo sana. KTN: " yatima wachanga kutoka kwenye mikono ya mama zao au vichanga wasio na baba kutoka kwa mama zao"

yatima

hii inarejea kwa watoto ambao hawana wazazi. Hata hivyo hapa neno hili limetumika kumaanisha watoto ambao hawana mama wla baba.

huchukua watoto kama dhamana kutoka kwa watu masikini

"huchukua watoto wa watu wa masikini ili kuhakikisha kuwa watu masikini watalipa pesa walizokopa"

dhamana

mwazimishaji anachukua kitu kutoka kwa mwazimaji ili kuhakikisha kwamba atalipa tena.

huzunguka

"kutembea huku na kule"

uchi pasipo mavazi

"uchi pasipo mavazi" maana yake ni sawa na kuwa uchi.

hubeba miganda ya nafaka ya wengine

hii inamaanisha wanfanya kazi kuzalisha chakula kwa wengine wala si kwa ajili yao wenyewe.

Job 24:11

Sentensi unganishi

Ayubu anaendelea kuongea

watu masikini hutengeneza mafuta

wanakamua zeituni ili kutoa mafuta ya zeituni

Ndani ya kuta wale watu waovu

"Kuta" inarejea nyumba nzima .KTN: " kwenye nyumba za wale watu waovu"

wanakanyaga mashinikizo ya divai ya watu waovu

wanazalisha shalibati ili kutengeneza divai.KTN: "wanakanyaga zabibu ili kutengeneza sjhalibati kwa ajili ya diva"

wenyewe huteseka kwa kiu

"huteseka kutokana na kiu au hupata kiu"

Job 24:13

Sentensi Unganishi

Ayubu anaendelea kuongea

huasi dhidi ya mwanga

maana ya mwanga

hawazijui njia zake, wala hawakai katika mapito yake

hii mistari miwili inaeleza kitu kile kile, na inatumika kwa pamoja kusisitiza kwamba hawataki kufuata njia ya mwanga. KTN: "hawajui jinsi ya kuishi maisha yenye maadili; hawataki kuisha maisha ya haki"

masikini na watu wahitajia

maneno "masikini" na "wahitaji" yanarejea kundi moja la watu na kusisitiza kuwa watu hawa ni watu ambao hawawezi kijisaidia wenyewe.

Job 24:15

Sentensi unganishi

Ayubu anaendelea kuongea

jicho la mzinzi

"jicho" linarejea binadamu kwa ujumla wake. KTN: "mzinzi"

kwa giza gaza

"kwenye machweo"

hakuna jicho litakaloniona

"jicho" hapa linarejea mwanadamu kwa ujumla wake.KTN: "hakuna mtu atakaye niona"

watu waovu huchimba kwenye nyumba

wanachimba ili kuiba kwenye hizo nyumba .

wao hujifungia wenyewe

"hujificha ndani"

maana kwao wote, giza nene ni kama asubuhi

giza nene ni faraja kwa waovu kama mwanga wa asubuhi kwa watu wa kawaida.

vitisho vya giza nene

"vitu vya kuogofya vinavyotokea usiku"

Job 24:18

Sentensi Unganishi

Ayubu anaendelea kuongea

kama povu juu ya uso wa maji

povu hudumu kwa muda mchache. Hii inasisitiza kuwa Mungu atasababisha waovu wapotee upesi.

sehemu ya ardhi yao imelaaniwa

KTN: "Mungu hulaani sehemu ya ardhi ambayo wanamiliki"

Kama ukame na joto huyeyusha...wale ambao wamefanya dhambi

Ayubu anasema kwamba wenye dhambi watapotelea kuzimu kwa njia ile ile kama vile theluji inavyoyeyuka na kupotea inapokuwa joto.

ukame na joto

haya maneno mawili yanaelezea hali ya hewa inayofanana.

Job 24:20

Sentensi Unganishi

Ayubu anaendelea kuongea

Tumbo

hii inarejea kwa mama. KTN: "mama"

minyoo itamla na kuona utamu

hii inamaana kuwa atakufa na minyoo itaula mwili wake. KTN: minyoo itafurahia kula mzoga wake" au "atakufa na mwili wake utaliwa na minyoo"

hatakumbukwa tena

" hakuna mtu atakayemkumbuka tena"

utavunjwa kama mti

" Mungu atawaharibu waovu kama mti"

mwovu huteketeza

sitiari hii inasisitiza jinsi mtu mwovu asivyofaa. KTN: "Kama mnyama mwitu anavyoua mawindo yake, ndivyo mtu mwovu huleta maumivu"

wanawake tasa ambao hawakuzaa watoto

watu wa wakati ule waliamini kuwa mtu ambaye hakuzaa watoto alikuwa amelaaniwa na Mungu. Hii inawakilisha wanawake wenye bahati mbaya kabisa.

Job 24:22

Sentensi Unganishi

Ayubu anaendelea kuongea

kwa nguvu zake

"kwa kutumia nguvu zake" au "kwasababu yeye ni mwenye nguvu"

huinuka na wala hawatii nguvu katika maisha

"wala hawatii nguvu katika maisha"maana yake Mungu hawaachi hai. KTN: "Mungu huinuka na hawapi watu waovu nguvu za kuishi" au "Mungu huinuka na kuwasababisha wafe"

bali macho yake yapo juu ya njia zao

hapa "macho" nirejea kwa Mungu. KTN: "lakini daima huangalia watendayo"

Job 24:24

Sentensi unganishi

Ayubu anaendelea kuongea

watashushwa

"Mungu atawashusha" au "Mungu atawaharibu"

watakusanywa kama wengine wote

baadhi ya tafsiri zingine zinasema "watanyauka na kufifia kama magugu"

watakatwa kama masuke ya nafaka

KTN:"Mungu atawakata kama mkulima anavyokata masuke ya nafaka"

Kama ndivyo, je ni nani anaweza kuthibitisha kuwa mimi ni mwongo ; nani anaweza kufanya maneno yangu yasifae kitu?

Ayubu anatumia swali hili kuonyesha uzito wa hoja yake. KTN: "hii ni kweli, hakuna mtu anaweza kuthibitisha kuwa mimi ni mwongo; hakuna wa kuthibitisha kuwa mimi ni mkosaji"

kufanya maneno yangu yasifae kitu?

"kuthibitisha ninachosema ni makosa"

Job 25

Job 25:1

Bildadi Mshuhi

hili ni jina la mtu kama ilivyo katika 2:11

Milki na hofu vipo pamoja naye

"naye" inarejea kwa Mungu. majina ya dhahania "milki" na "hofu" yanaweza kutajwa kama vitenzi. KTN: "Mungu ni mtawala wa yote, na watu wanapaswa kumhofu yeye peke yake"

katika sehemu zake za juu mbinguni

"katika mbingu" au "kwenye mbingu juu"

Je kuna ukomo wa idadi ya majeshi yake?

Bildadi anatumia swali hili kueleza jinsi Mungu alivyo mkuu. KTN: "Hakuna ukomo wa idadi ya malaika katika jeshi lake" au Adui zake ni wakubwa sana kwamba hakuna awezaye kuwahesabu"

je ni juu ya nani mwanga wake haumuliki?

Bildadi anatumia swali hili kueleza kwamba Mungu hutoa mwanga kwa kila mtu. KTN: "Wala hapana mtu ambaye mwanga wake haumuliki" au "Mungu hufanya mwanga wake kung'aa juu ya kila mmoja"

Job 25:4

Sentensi Unganishi

Bildadi anaendelea kuongea.

Mtu anawezaje ... Mungu? Je anawezaje aliyezaliwa ... kwake?

maswali haya mawili yematumika pamoja kusisitiza kwamba haiwezekani kwa mtu mwema kiasi cha kutosha mkwa Mungu

Basi mtu anawezaje kuwa mwenye haki kwa Mungu?

"Mtu hawezi kuwa mwenye haki kwa Mungu"

Je anawezaje yeye aliyezaliwa... kukubalika kwa Mungu?

" yeye ambaye amezaliwa na mwanake hawezi kuwa msafi au kukubalika kwake"

nyota si safi kwenye macho yake

"safi" maana yake "kamilifu" KTN: "anafikiri hata nyota hazina ukamilifu"

Jinsi gani mtu ... mwana wa mtu, ambaye ni mnyoo

hii mistari miwili inasema jambo moja na inatumika pamoja kukazia kuwa mtu si mkamilifu.

ambaye ni mnyoo

Bildadi anaeleza kwmba mwanadamu ni wa thamani ndogo kama minyoo. KTN: "ambaye hana thamani kama mnyoo"

mwana wa mtu

hii ni namna nyingine ya kumaanisha mtu. KTN: "Mtu"

Job 26

Job 26:1

jinsi gani ulimsaidia yule ...mkono ambao hauna nguvu!

Ayubu anamshutumu Bildadi. Neno "yule" linamrejea yeye mwenyewe (Ayubu). KTN: "Mimi sina uwezo wal nguvu, lakini unajifanya kama umenisaidia- ukweli ni kwamba hujanisaidia kabisa!"

mkono ambao hauna nguvu

Ayubu anajielezea mwenyewe kuwa..."mimi, ni kama mkono ambao hauna nguvu au "yule ambaye ni dhaifu kabisa"

Jinsi gani umemshauri yule asiyekuwa na hekima na kumtangazia maarifa ya kweli!

Ayubu anasema kwamba Bildadi hajatoa ushauri mzuri wala maarifa kwake. KTN: " Umetenda kana kwamba hauna maarifa kwa njisi ulivyonishauri"

kumtangazia maarifa ya kweli

"kumpa ushauri mzuri"

Kwa msaada wa nani umeongea maneno haya? je ilikuwa roho ya nani... yako?

katika maswali haya Ayubu anaendelea kumdhihaki Bildadi. KTN: "lazima ulipata msaada kuongea maneno haya. Yamkini roho fulani ilikusaidia kuyaongea maneno haya"

Job 26:5

waliokufa

" wale ambao walikufa" au " roho za wafu"

tetemeka

wanatetemeka kwa sababu wanamwogopa Mungu. KTN: "kutetemeka kwa hofu" au "kutetemeka kwa hofu ya Mungu"

wale ambao wapo chini ya maji

Hii inaelezea watu waliokufa ambao hutetemeka"

wote wanaoishi ndani yake

hii nazungumzia kuhusu watu waliokufa ambao hutetemeka. neno "yake" linamaanisha kwenye maji

kuzimu ipo tupu mbele za Mungu; uharibifu mwenyewe hauna kifuniko

kuzimu inaongelewa kana kwamba ni mtu. kuwa "tupu" au kukosa" kifuniko" ni kuwa wazi kabisa na kushindwa kuficha chochote. KTN: " Ni kama kuzimu ilivyo wazi mbele za Mungu, maana hakuna kitu kuzimu, au sehemu ya uharibifu ambayo imejificha kwa Mungu"

uharibifu

hili ni neno jingine kumaanisha kuzimu. KTN: "sehemu ya uharibifu"

Job 26:7

hulinyosha anga la kaskazini juu ya nafasi wazi

anga la kaskazini linawakilisha mbingu, sehemu ambapo Mungu huishi pamoja na viumbe alivyoviumba huko.

huyafunga maji kwenye mawingu yake mazito

mawingu yanazungumziwa kana kwamba ni bulanketi kubwa ambapo Mungu huyafunga maji ya mvua. KTN: "Huyafunga maji katika mawingu yake mazito"

walakini mawingu hayapasuki chini yake

KTN: "Lakini uzito wa maji haupasui mawingu"

Job 26:9

na hutandaza mawingu yake juu yake

maneno haya yanasema jinsi huifunika sura ya mwezi. KTN: " kwa kutandaza mawingu yake mbele yake"

amechonga mpaka wa duara

Anasema kana kwmba Mungu aliweka alama ya mpaka juu ya bahari.

Job 26:11

Nguzo za mbingu hutetemeka na kustaajabu kwa kukemea kwake

Ayubu anaongelea watu kama nguzo ambazo hutetemeka kwa hofu wakati Mungu anapokasirika.

alimvunjavunja Rahabu

alimharibu Rahabu

Rahabu

Hili ni jina la kiumbe cha kutisha kilichoishi katika bahari.

Job 26:13

Kwa pumzi yake alisafisha anga

"pumzi" au "puliza" ni sura ya kuwakilisha kitendao cha Mungu kusababisha upepo yayasukume mawingu. KTN: " Kwa pumzi, Mungu alisafisha anga" au "Mungu aliyapuliza mawingi hata anga likawa safi"

mkono wake ulimemchoma nyoka mwenye kukimbia.

"mkono wake" unawakilisha upanga wa Mungu na 'kumchoma' linawakilisha mauaji. KTN: "Kwa upanga wake alimchoma nyoka mwenye kukimbia"

nyoka mwenye kukimbia.

" nyoka huyu alikuwa anajaribu kumtoroka" zingatia 26:11

Tazama, walakini hivi ni viunga vya njia zake

Hapa "viunga" vinawakilisha sehemu ndogo ya kitu kikubwa inayoweza kuonekana.KTN: "Tazama vitu hivi ambavyo Mungu amavifanya vinaonyesha sehemu ndogo sana ya uwezo wake mkuu"

ni mnong'ono mdogo kiasi gani tunasikia kutoka kwake

KTN: " Tunasikia tu mnong'ono wake wa utulivu"

ni nani anawezakufahamu ngurumo ya nguvu zake?

"ngurumo ya nguvu zake" inawakilisha ukuu wote wa yale anayoyafanya Mungu. Ayubu anaelezea kuwa nguvu za Mungu ni kuu sana kiasi kwamba hakuna mtu mwenye kuzifahamu. KTN: "hakuna mwenye kufahanu ukuu wa nguvu zake"

Job 27

Job 27:1

Hakika kama Mungu anavyoishi

Hii ni namna ya dhati ya kuweka ahadi. KTN: "Ninaapa kwa Mungu"

ameniondolea haki yangu

kuindoa haki inamaanisha kukataa kumtendea haki Ayubu

aliyefanya maisha yangu kuwa machungu

"amesababisha niwe na uchungu" au " amenifanya nikasirike kwa sababu alinitendea kwa namna isiyo nzuri"

wakati uhai wangu ukiwa ndani yangu

hii inamaana ya maisha yake yote. KTN: wakati wote ambapo uzima wangu ukiwa ndani yangu" au "kwa muda wote ambao uhai wangu bado upo ndani yangu"

pumzi kutoka kwa Mungu puani mwangu

pumzi puani inawakilisha uwezo wa kupumua, "pumzi kutoka kwa Mungu" inawakilisha kitendo cha Mungu kumfanya aweze kupumua. KTN: "Mungu ananiwezesha kupumua"

puani

"pua"

Job 27:4

Hakika midomo yangu haitanena uovu, wala ulimi wangu kusema uongo

"midomo yangu" na "ulimi wangu" vifungu hivi vyote vina maana moja na vimetumika kusisitiza kwamba Ayubu hatasema mambo yasiyofaa. KTN: "Hakika sitasema ouvu au uongo"

haitanena uovu...kusema uongo

"uovu" na "uongo" ni majina dhahania yanayoweza kuelezea "kwa uovu" na "kwa udanganya" KTN: "kunena kwa uovu... kusema kwa udanga udanganyifu"

Sitakubali kwamba ninyi watatu mpo sahihi

"sitakubaliana nanyi na kusema kwamba ninyi watatu mpo sahihi"

sitaukana uadilifu wangu

"sitaacha kusema ya kwamba mimi si mwenye hatia" au " daima nitasema ya kuwa mimi mwadilifu"

Job 27:6

nashikamana na haki yangu

" mimi nimedhamiria kuendelea kusema ya kwamba ni mwenyehaki"

sitaiacha

" sitaacha kusema kuwa mimi ni mwenye haki"

mawazo yangu hayatanisuta

"hata katika mawazo yangu sitajishutumu mwenyewe"

Adui yangu awe...yule anayeinuka dhidi yangu awe

hivi vishazi viwili vina maana moja. Vinaonyesha hamu ya Ayubu kutaka jambo hili litokee

Adui yangu na awe kama mtu mwovu

" Adui yangu na aadhibiwe kama mtu mwovu " au "Mungu amuadhibu adui yangu kam anavyowaadhibu watu waovu"

Yule ainukaye dhidi yangu na awe kama mtu asiye haki

" yule anyeinuka kinyume nami aadhibiwe kama mtu asiye haki"

yeye ainukaye dhidi yangu

"Yeye anayenipinga" au " mshitaki wangu"

Job 27:8

Maana ni nini tumaini la mtu kafiri wakati... wakati Mungu aondoapo uzima wake?

" hakuna tumaini kwa mtu kafiri wakati Mungu... aondoapo roho yake."

wakati Mungu amwondoapo, wakati Mungu aondoapo uzima wake

misemo yote miwili inamaana moja.KTN: "Wakati Mungu anapomkatilia mbali na kuondoa uzima wake" au "wakati Mungu anaposababisha afe"

amwondoapo

"anapomwua" au " aposababisha afe"

aondoapo uzima wake

"anapomwua" au " anapomfanya asiendelee kuishi"

Je Mungu atasikia kilio chake wakati taabu itakapokuja juu yake?

"Mungu hatasikia kilio chake wakati taabu itakapokuja juu yake" au " Wakati taabu itakapokuja juu yake na kulilia msaada, Mungu hatamsikia."

Mungu atasikia kilio chake

"Mungu atamwitikia kilio chake"

Je atamfurahia Mwenyezi na kumwita Mungu katika nyakati zote?

Ayubu anatumia swali hili kusema kuwa mtu kafiri hatamfurahia Mwenyezi na kumwita Mungu katika nyakati zote. au " hatayafurahia matendo ya Mwenyezi na wala hata mwomba Mungu mara kwa mara"

Job 27:11

nitawafundisha

"nitawa.." ni neno katika wingi kumaanisha marafiki watatu wa Ayubu.

mkono wa Mungu

Mkono wa Mungu unawakilisha nguvu zake. KTN: "Nguvu za Mungu"

Sitayaficha mawazo ya Mwenyezi

"mawazo" ni jina dhahani ambapo laweza dhahiri pamoja na kitenzi "fikiri".KTN: "Sitawaficha yale ambayo Mwenyezi hufikiri"

basi mbona mmeongoa upuuzi huu wote?

Ayubu anatumia swali hili kuwakemea arafiki zke kwa kuongea vitu vya kipumbavu. KTN: "walakini mmeongea upuu huu wote" au " Haikuwapasa kuongea kwa upumbavu"

Job 27:13

Hii ndiyo hatima ya mtu mwovu kwa Mungu

Hatima ya mtu mwovu kwa Mungu inahusiana na mpango wa Mungu kwa mtu huyo. KTN: " huu ndio mpango wa Mungu kwa mtu mwovu"

urithi wa mnyonyaji ambao hupokea kutoka kwa Mwenyezi

"urithi wa mnyonyaji" ni stiari kuonyesha kitu gani kitatokea kwa mnyonyaji. Mambo atakayopokea toka kwa Mungu yanaongelewa kama ndiyo urithi wake.

ni kwa ajili ya upanga

"watakufa katika mapigano"

Job 27:15

wale ambao husalia

Hii inahusu watoto wa mtu mwovu ambao huendelea baada ya baba zao kufariki. KTN: "Wale ambao huendelea kuishi baada ya baba zao waovu kufariki"

watazikwa kwa tauni

"watakufa kwa tauni"

wajane wao... yao

maneno "wao... yao" yanahusu wale watakaosalia, ambao ni watoto wa mtu mwovu

hurundika fedha kama mavumbi

"hurundika "maana yake hukusanya sana. Ayubu anasema kuwa ilikuwa rahisi kwa mtu huyu kujipatia fedha kama vile mavumbi.

hurundika mavazi kama udongo

"hurundika "maana yake hukusanya sana. Ayubu anasema kuwa ilikuwa rahisi kwa mtu huyu kujipatia mavazi kama vile kuzoa udongo.

Job 27:18

Huijenga nyumba yake kama buibui

" kama buibui ajengavyo mifumo yake"

Huijenga nyumba yake kama buibui

" kama buibui ajengavyo mifumo yake"

kama kibanda

kibanda ni nyumba ya muda ambayo si imara. KTN: "Kama kibanda cha muda mfupi"

hulala chini kitandani akiwa tajiri

" analala wakati wa usiku akiwa tajiri"

walakini hawezi kuendelea kufanya hivyo

"walakini hataendelea kulala kwenye kitanda akiwa tajiri" au "hataendelea kuwa tajiri"

hufumbua macho yake

"ataamuka"

na kila kitu kimetoweka

"utajiri wake wote utaondoka" au "kila kitu kitakuwa kimepotea"

Job 27:20

vitisho humkabili

" mambo ya kutisha humtokea kwa ghafula" au "ghafula atashikwa na woga"

kama maji

" kama mafuriki" au "kama maji jaa upesi"

dhoruba humtoa

"upepo mkali humpeperusha mbali"

humfagia mbali na sehemu yake

"upepo humfagia mbali na sehemu yake kama mwanamke anafagia uchafu kwenye nyumba" au " upepo humpeperusha kwa urahisi mbali na sehemu yake"

sehemu yake

"nyumba yake"

Job 27:22

Maelezo ya Jumla

mistari ya 22-23 Ayubu anazungumzia upepo kana kwamba ni mtu mwenye kumshambulia mtu mwovu

unajirusha wenyewe juu yake

hapa "unajilisha wenyewe " inamaanisha upepe. "unavuma kwa nguvu dhidi yake kama mtu mwenye kumshambulia"

anajaribu kuukimbia mko wake

" anajaribu kukimbia kutoka katika mamlaka yake"

Anapiga makofi yake kwa kumdhihaki.

" Upepo unato sauti kubwa kama ya mtu anayepiga makofi ili kudhihaki"

anazomewa mbali na sehemu yake

"amepeperushwa mbali na sehemu yake na anazomewa kwa dhihaka"

Job 28

Job 28:1

machimbo

hii ni sehemu ambapo watu huchimba miamba kwenye ardhi. Hii miamba inachuma ndani yake.

husafisha

mchakato wa kupasha joto chuma ili kuondoa uchafu wote ndani yake.

chuma huchukuliwa kwenye ardhi

"watu huchukua chuma kutoka kwenye ardhi"

shaba huyeyushwa kutoka kwenye mawe

" watu huyeyusha shaba kutoka kwenye mawe" au "watu huchoma mawe kuyeyusha shaba ndani yake"

shaba

chuma cha brauni ambacho ni muhimu

yeyusha

huu ni mchakato wa kuchoma miamba ili kuyeyusha madini ndani yake na kutoa madini hayo kwenye miamba

Job 28:3

Binadamu hukomesha giza

huweka nuru mahali penye giza. Watu waliweza kutumia miale, ama taa au tochi.KTN:" Bibadamu hubeba mwanga kwenye sehemu za giza"

kwenye mpaka wa mbali zaidi

"kwenye sehemu za mbali zaidi kwenye machimbo"

uvunguvungu ...giza nene

haya mafumbo mawili yametumika kuonyesha kuwa giza ni kuu sana

shimo

tundu jembambale lenye kina linalochimbwa ardhini au kwenye mwamba. Watu hushuka chini ya tundu ili kuchimba.

sehemu ambazo zimesahauliwa na mguu wa mtu yeyote

KTN: " ambapo hakuna mtu amewahi kupakanyaga"

Huning'inia mbali na watu

KTN:" Mbali na watu huning'inia kwenye kamba ndani ya shimo"

Job 28:5

ardhini ambamo hutoka mkate

mkate unawakilisha chakula kwa ujumla. chaakula hutoka kwenye ardhi ni sitiari kwmab chakuka hukua kwenye ardhi. KTN: "ardhini ambapo chakula hustawi"

hugeuzwa chini kama kwa moto

hii inaweza kumaanisha 1) watu waliwasha moto chini ardhi ili kubomoa sehemu za mwamba 2) huboma chini sana kama kwamba kuteketeza kwa moto"

hugeuzwa...mawe yake ...vumbi lake

maneno yake, lake yanamaana ya ardhi

Johari

neno hili linamaana ya jiwe la bluu lenye thamani sana.

Job 28:7

Hakuna ndege mbua aijuaye njia yake ... wala hakuna jicho la tai halijaiona

KTN: "Hakuna ndege mbua au tai anayeijua au akwisha kuiona njia anayokwenda kwenye mgodi"

ndege mbua

ndege alaye wanyama wangine

tai

kipanga

wanyama wenye kujivuna hawajapita kwenye njia kama hiyo...wala simba mwenye hasira hajapita pale

Virai hivi vinaeleza maana zenye kufanana

wanyama wenye kujivuna

hii inamaanisha wanya mwitu wenye nguvu

Job 28:9

Binadamu huulaza makono wake juu ya mwamba mgumu

hii inamaanisha kupasua mwamba.KTN: "huchimba kwenye mwamba mgumu"

mwamba mgumu

" mwamba gumegume"

huipindua milima kwenye mizizi yake

"huipindua milima juu chini kwa kuvuita mizizi yake"

macho yake huona

"huona"

Huifunga mifereji ili istiririke

kuifunga mifereji inakilisha kuzuia majia au kuizuia mifereji ya maji.

kilichofichwa pale

hii inarejea vitu ambavyo watu hawawezi kuviona kwa sababu vipo chini ya ardhi au chini ya maji.

Job 28:12

Maelezo ya Jumla

kwenye 28:12-28, hekima na maarifa vimesemwa kama vitu ambavyo vipo mahali fulani na watu wanataka wavipate. kutafuta hekima na maarifa inawakilisha kuwa na busara na kujifunza kufahamu vitu kwa uzuri.

Je hekima itapatikana wapi? Je ni sehemu gani yenye maarifa?

Maswali haya yanamaana moja na yametumika kuonesha kuwa ni vigumu kupata hekima na maarifa.

Je hekima itapatikana wapi? Je ni sehemu gani yenye maarifa

Kuwa mwenye hekima na maarifa inazungumziwa kana kwamba ni kutafuta hekima ana maarifa: KTN: "Jinsi gani watu huwa na hekima? Jinsi gani watu hujifunza kufahamu vitu kwa uzuri?"

Binadamu hajui thamani yake

Hapa inaweza kumaanisha kuwa:- 1) "Watu hawajui uzuri wake" au 2) "Watu hawajui mahali ilipo"

wala haipatikani katika nchi ya walio hai

nchi ya walio hai inamaana ya ulimwengu huu ambapo watu wanaishi. KTN: "na hakuna mtu anayeweza kupata hekima katika ulimwengu huu "

Maji yenye kina... yanasema, 'haiapo ndani kwangu' bahari inasema, ' haipo kwangu'

vilindi vya maji na na bahari vinasimama kama watu wanaoweza kuongea. KTN: "Hekima haipo ndani ya vilindi vya maji chini ya ardhi, wala katika bahari"

Job 28:15

Haiwezi kupatikana kwa dhahabu

Hii inamaanisha kuwa hekima ina anathamani zaidi kuliko dhahabu. KTN: "Watu hawawezi kulipa dhahabu kwa ajili ya kupata hekima"

wala fedha haiweza kupimwa kwa thamani yake

Hii ina maana kwamba hekima inathamani sana kuliko fedha. KTN: "na watu hawawezi kupima fedha za kutosha ili kulipa kwa ajili ya hekima"

Haiwezia kuthaminishwa kwa ... johari

hii inamana kuwa hekima inathamani zaidi ya dhahabu ya ofiri, inathamani kuliko oni na johari.

ofiri

Hili ni jina la eneo ambako kulikuwa na dhahabu safi.

oni

jiwe jeusi lenye thamani

johari

jiwe la bluu lenye thamani sana.

Dhahabu na fuwele haziwezi kulingana nayo kwa thamani

Hapa inamaana kuwa hekima inathamani zaidi kuliko dhahabu na fuwele.

fuwele

jiwe la thamani lililo safi au angavu kwa rangi yake.

wala haiwezi kubadilishwa kwa kito cha dhahabu safi

na haiwezi kubadilishwa kwa kito cha dhahabu safi." Hii inamaana kuwa hekima ina thamani zaidi kuliko kito cha dhahbu safini.

kubadilishwa

"kuuzwa"

Job 28:18

Fedhalika au marijani havistahili kutajwa

"haifai kutaja marijani au fedhaluka" hii inamaan kuwa hekima inastahili zaidi kuliko marijani na fedhaluka wala Ayubu hahitaji kusema chochote juu ya hivi.KTN: "Sitajisumbua kutaja marijani au fedhaluka" au marijani na fedhaluka havina thamani vikilinganishwa na hekima"

marijani

Ni kitu kizuri na kigumu ambacho hustawi chini ya bahari.

fedhaluka...rubi...topazi

Haya ni mawe yenye thamani sana

topazi ya Ethiopia haiwezi kulingana nayo

Hii inamaanisha kwamba hekima inathamani zaidi kuliko topazi.

wala haiwezi thaminishwa kwa vigezo vya dhahabu safi

"na hekima haiwezi kuthaminishwa kwa vigezo vya dhahabu safi" hekima inathamani zaidi ya dhahabu safi.

Job 28:20

Basi, hekima hutoka wapi? Mahali pa ufahamu ni wapi?

Ayubu anatumia maswali haya kudokeza jinsi gani watu hupata ufahamu na hekima> KTN: " Nitawaambia hekima hutoka wapi na mahali ufahamu ulipo" au "nitawaambia jinsi ya kuwa na busara na namna ya kujifunza vitu vya ufahamu"

Basi hekima hutoka wapi

hekima inaongelewa kana kwamba ipo mahali fulani na huwajia watu. hii inamaanisha watu kujipatia busara. KTN: "Basi watu hupata wapi hekima" au "basi namna gani watu hupata busara"

Mahali pa ufahamu ni wapi

Ufahamu umeongelewa kama kitu ambacho kipo hali. KTN: "Watu hupata wapi ufahamu" au "namna gani ya watu hufahamu vitu"

hekima imefichwa kutoka kwenye macho ya viumbe hai vyote

Viumbe hai haviwezi kuiona hekima. KTN: "Hakuna kiumbe hai chenye kuweza kuiona hekima"

na imefichwa kutoka kwa ndege wa mbinguni

"hata ndege ambao huruka katika anga hawawezi kuona hekima"

uharibifu na mauti husema

hapa "uharibifu" na "mauti" ni tamathali kwa sehemu ambapo watu huelekea wakati wanapofariki.

Job 28:23

Mungu inaifahamu njia yake; anapajua mahali pake

"Mungu anajua jinsi ya kuipata hekima. Anajua mahali ilipo"

miisho ya nchi

"sehemu za mbali za dunia"

aliyagawa maji kwa vipimo

Mungu hufanya maamuzi ni maji kiasi gani yanapaswa kuwepo kwa kila sehemu. KTN: "aliamua ni maji kiasi gani yanapaswa kuwepo kwa kila sehemu" au "ameweka kiwango cha maji ambacho alikipanga kwa kila sehemu"

Job 28:26

na njia kwa mwanga wa radi

maana yaake 1) aliamua namna yamapigo ya mwanga au 2) aliamua mahali pa kuelekea ngurumo za radi.

Hofu ya Bwana -ni hekima

"hofu" au "heshima" KTN: " ukimheshimu Bwana- utakuwa na busara"

kujitenga na uovu ni ufahamu

KTN: "Kukataa kutenda vitu viovu ni ufahamu" au " kama utaepuka kutenda vitu viovu, utaweza kufahamu mambo vizuri"

Job 29

Job 29:1

La, ningekuwa kama nilivyokuwa katika miezi iliyopita

"nitamani ningekuwa kama nilivyikuwa katika miezi ya kale"

wakati taa yake ilipong'aa juu ya kichwa changu

Taa ya Mungu kung'aa juu Ayubu inawakilisha Mungu kumbariki Ayubu. KTN: "Wakati baraka za Mungu zilipokuwa kama taa iking'aa juu ya kichwa changu"

wakati nilipotembea gizani kwa nuru yake

kutembe kwenye giza inawakilisha kukabiliwa na hali ngumu"

Job 29:4

katika kukomaa kwa siku zangu

"nilipokwa kijana na mwenye nguvu"

wakati urafiki na Mungu ulikuwa kwenye hema yangu

" Wakati Mungu alipokuwa rafiki yangu na alipoilinda nyumba yangu"

wakati njia yangu ilipooshwa katika malai

"wakati njia yangu ilipomiminika malai" au "wakati ng'ombe wangu walipotoa malai kwa wingi"

na mwamba ulinimiminia mito ya mafuta

" watumishi wangu walipo kamua mafuta ya mizeituni kwa wingi" au " wakati ambapo mafuta yalitiririka kama mito kutoka kwenye mwamba wa kusindikia"

Job 29:7

viunga vya mji

Hili ni eneo wazi katika kijiji au mji ambapo ni makutano ya miji miwili au zaidi.

waliinuka na kusimama kwa ajili yangu

hii ni alama ya heshima.KTN: "waliinuka na kusimama kwa kuniheshimu"

Job 29:9

nipokuja kwa wafalme wajizuia kuongea

hii ilikuwa alama ya heshima

waliweka mkono wao juu ya kinywa chao

hii ilikuwa alama ya heshima. Walifanya hivi kuonesha kuwa usingeweza kuongea.

sauti za waungwana zilinyamaza

"waungwana walinyamazisha sauti zao" au "waungwana waliacha kuongea"

na ulimi wao gandamana kwenye makaakaa ya vinywa vyao

maana yake walimweshimu Ayubu hadi kukosa neno la kusema. KTN: " walijihisi kushindwa kuongea" au "na hawakuwa na jambo lolote la kusema"

Job 29:11

baada ya masikio yao kunisikia.... baada ya macho yao kuniona

masikio yanawakilisha wale waliomsikia na macho yanawakilisha wale waliomwona. KTN: "baada ya kusikia nilichowaeleza ... baada ya kuniona"

waliweza kunishuhudia na kunithibitisha

"waliweza kunishuhudia kwa kunithibitisha"

nilimwokoa mtu masikini aliyenililia

Hapa"mtu masikini" inahusu mtu yeyote ambaye ni masikini. KTN: "niliwaokoa watu masikini ambao walinililia"

Baraka ya yule aliyekuwa karibu kupotea ilinijia

baraka ya mtu kwenda kwa mwingine inawakilisha kitendo cha huyi mtu kumbariki mwingine.KTN: "yule aliyekuwa karibu kupotea aliweza kunibariki"

yeye aliyekuwa karibu kuangamia

Mtu yeyote aliyekuwa anakaribia kufa. KTN: " wale ambao walikaribia kufa"

nilisababisha moyo wa mjane kuimba kwa furaha

"moyo wa mjane" inamaana ya mjane yoyote. KTN: "Niliwafanya wajane waimbe kwa furaha kuu"

Job 29:14

Nilivaa haki, nayo ikanifunika

watu wa wakati ule waliongelea haki kama vazi. KTN: "Nilitenda haki, nayo ikawa kama vazi la kujisitiri juu yangu"

uadilifu wangu ulikuwa kama joho na kilemba

watu wa wakati ule waliongelea uadilifu kama vazi. KTN: "Nilitenda kwa adili, na ilikuwa kama joho na kilemba juu yangu"

kilemba

vazi refu ambalo wanaume hufunga kuzunguka vichwa vyao, huvaa kama kofia.

nilikuwa macho kwa watu vipofu

Hii inamaanisha kuwasaidia watu vipofu. KTN: "nilikuwa kama macho kwa ajili ya watu vipofu" au "niliwaongoza watu vipofu"

nilikuwa miguu kwa watu viwete

"nilikuwa kama miguu kwa watu viwete" au "niliwasaidia watu viwete"

nilikuwa baba kwa watu wahitaji

hapa neno baba linawakilisha kutoa kwa ajili ya watu. KTN: "Nilitoa kwa ajili ya watu wahitaji kama baba anavyotoa kwa ajili ya watoto wake"

Job 29:17

Maelezoa ya jumla

katika mistari ya 18-28 Ayubu anasimulia mambo ambayo alifanya kabla mambo mabaya hajatokea kwake.

nilivunja taya za ... nilimng'oa mwathirika

" niliwafanya dhalimu waache kuwatesa watu, kam mtu anayevunja taya la mnyama mwitu na kuokoa mhanga kutoka katika meno yake"

nitakufa katika kiota changu

" nitakufa kwenye nyumba yangu pamoja na familia yangu" au "nitakufa katika usalama wa nyumbani kwangu"

nitazidisha siku zangu kama mchanga

"nitaishi maisha marefu" au "nitaishi miaka mingi "

Mizizi yangu ... matawi yangu

Ayubu anaongea juu ya nguvu zake, anasema yeye ni kama mti imara uliomwagiliwa vizuri.

Job 29:20

heshima ndani yangu ni mpya siku zote

"watu hunipa heshima daima" au "watu huniheshimu mara kwa mara"

upinde wa nguvu zangu ni mpya daima mkononi mwangu

"siku zote nipo imara kama upinde mpya"

hotuba yangu ilidondoka kama maji juu yao

"hotuba yangu burudisha mioyo yao kama matone ya maji yanavyoburudisha miili ya watu" au nichosema kwao kiliwaburudisha kama matone ya maji"

Job 29:23

walinisubiri daima kama walivyosubiri mavua

watu walimsubiri kwa subira na kutarajia kusikia mambo mema.

"walisubiri kwa hamu niongee ili wanufaike kutoka katika usemi wangu"

kama walivyofanya kwa mvua ya masika

"wakulima walisubiri kwa hamu mvua ya masika"

mvua ya masika

mvua ya masika

hii ni mvua kubwa ambayo hunyesha kabla ya majira ya ukame

nilitabasamu kwa ajili yao

"nilitabasamu kwa aji yao ili kuwafariji"

mwanga wa uso wangu

hii inawakilisha ukarimu waliouna katika sura ya Ayubu

Job 29:25

niliwachagulia njia zao

hii inamaanisha kuwaamulia jambo wanalopaswa kutenda

niliketi kama mkuu wao

"niliwaongoza kama mkuu wao"

niliishi kama mfalme kwenye jeshi lake

watu walimtii Ayubu kama mfalme na walikuwa kama jeshi lake.

nilikuwa kama mtu anayewafariji waombolezaji

"niliwafariji wakati wa kuomboleza kwao"

Job 30

Job 30:1

hawana kitu lakini mdhaha kwa ajili yangu

"hunidhihaki tu"

ambao baba zao nigewakataza kufanya kazi sambamba na mbwa wa kundi langu

"ambao baba zao niliwadharau na sikuwaruhusu kufanya kazi sambamba na mbwa wa kundi langu"

mbwa wa kundi langu

"mbwa ambao walilinda kundi langu"

Je nguvu za mikono ya baba zao zingewezaje kunisaidia mimi... zimeharibika?

"nguvu za mikono ya baba zao hazikunisaidia kunisaidia mimi... zimeharibika"

watu ambao nguvu zao za ukomavu wa umri wa o zimeharibika

"watu ambao wamezeeka na hawana nguvu" au "watu ambao wamekuwa wazee na dhaifu"

walikonda kwa umasikini na njaa

neno "wali.." ni kiambishi kwa kumaanisha baba wa vijana wenye dhihaka.

walikonda kwa umasikini na njaa

"walikonda sana kwa sababu walikuwa masikini na hawakupata mahitaji ya kutosha"

tafuna kwenye ardhi kavu

"walitafuna mzizi waliyoipata katika ardhi" au "kutafuna kwenye ardhi kavu" ni picha kuwa walikula chochote walichoweza kukipata katika ardhi kavu"

Job 30:4

Sentensi Unganishi

Ayubu anaendelea kuongea kuhusu baba zao wenye kudhihaki

mboga ya chumvi ...majani ya vichakani...mizizi ya miretemu

Hii ni mimea ambayo watu waliweza kula endapo hawakuwa kupata chakula kizuri.

mizizi ya miretemu kilikuwa chakula chao

(1) watu walikula mizizi ya miretemu au 2) watu waliota moto kwa kuchoma mizizi ya miretemu.

walifukuzwa kutoka kati ya watu ambao waliwapigia kelele... mwizi

"walipigiwa kelele na watu ...mwizi na kulazimishwa kuondoka"

waliwapigia kelele kama mtu anavyompigia kelele mwizi

"waliwapigia kelele kana kwamba walikuwa wezi"

Job 30:7

walilia kama punda

"walilia kwa kupata njaa"

walikuwa uzao wa wapumbavu, naam, wa watu wasiofaa

"walitenda kama watu wasiokuwa na akili"

walifukuzwa kwa mijeredi watoke kwenye nchi

"walifukuzwa watoke nje ya nchi kama waharifu"

Job 30:9

hawaachi kunitemea mate usoni

"hata hunitemea mate usoni"

Mungu amelegeza kamba ya upinde wangu na kunitesa

"Mungu ameziondoa nguvu zangu kwa ajili ya kujitetea mwenyewe"

Job 30:12

juu ya mkono wangu wa kuume huinuka umati

"kundi la vijana hushambulia nguvu zangu" au " makundi ya watu wanashabulia heshima yangu"

hujikusanya dhidi yangu kwa kunizunguka

...adui wamejiandaa kumshambulia Ayubu, kama jeshi linavyojiandaa kushambulia...

Job 30:14

kama jeshi kwenye ufa mpana katika ukuta wa mji

Ayubu analinganisha hali yake na mji ambao upo katika mashambulizi wakati ukuta wake wa ulinzi unaufa

heshima yangu imefukuziwa mbali kama kwa upepo

"upepo umepeperusha heshima yangu"

mafanikio yangu yanatoweka kama wingu

Mali ya Ayubu imepotea kama wingi ambalo huonekana ghafula na hutoweka kutoka angani.

Job 30:16

Sasa uhai wangu unamiminika kutoka ndani yangu

Ayubu anahisi yu karibu kufa

maumivu ambayo yanaguguna kwangu hayapumziki

Ayubu anaongelea maumivu yake kam kitu chenye uhai.

Job 30:18

amenitupa kwenye matope

Ayubu anasema amefedheheshwa na Mungu

Job 30:20

katili

neno hili linamaana ya kukosa huruma

kwa nguvu za mkono wako umenitesa

Neno "mkono" linawakilisha nguvu za Mungu

Job 30:22

unaniinu juu kwenye upepo ...unanirusha nyuma na mbele katika dhoruba

Hii inaelezea mateso makuu ambayo Mungu amfanya Ayubu avumilie

nyumba ya hatima kwa viumbe hai vyote

"nyumba" inawakilisha sehemu ambapo wafu huelekea

viumbe hai vyote

vitu vyote vilivyo hai kwa sasa lakini vitakufa siku moja

Job 30:24

je hapana mtu wa kufikisha mkono wake kuomba msaada wakati anapoanguka? Je mtu mwenye shida hawezi kuomba msaada?

(1) "Niliwasaidia watu ambao walianguka wakati waliponiomba msaada . Niliwasaidia waliokuwa na taabu walipoomba msaada". au (2) "Nimeanguka na Mungu hapaswi kuona kama ninakosea ninapoomba msaada wake. Niko kwenye shida, naomba msaada!"

Je sikulia...shida? Je sikusononeka...mtu?

"Unajua kwamba nililia ...shida, na nilisononeka ...mtu!"

Nilisubiri mwanga ...giza likaja

Hapa "mwanga" unawakilisha baraka na kibali cha Mungu na "giza" linawakilisha shida na mateso.

Job 30:27

Moyo wangu umetaabika na wala haupumziki

Ayubu anaongelea moyo wake kama ni mtu

Ninarandaranda na ngozi yenye giza lakini si kusababu ya jua

"Daima nipo katika hudhuni na giza"

ndugu wa mbwa mwitu, mshirika wa mbuni

Ayubu anafananisha mateso yake na kuomba kwake msaada kama kilio cha mbweha na mbuni.

Job 30:30

Mifupa yangu imeungua kwa joto

Hapa "mifupa" inawakilisha mwili wote, ambao unaugua katika homa

maombolezo

"maombolezo" ni sauti kuu ya kilio chenye huzuni au maumivu.

Job 31

Job 31:1

Maelezo ya jumla

Ayubu anaendelea kuzungumza

Nimefanya patano na macho yangu

"Nimejiahidi mwenyewe kwamba sitamwangalia mwanamke kwa tamaa"

kwa namna gani tena napaswa kumtazama mwanamwali kwa tamaa?

Ayubu anatumia swalli ili kutia mkazo kwamba hatavunja ahadi yake.

Ni sehemu gani kutoka kwa Mungu juu, na urithi gani kutoka kwake mwenye nguvu aliye juu?

sentensi hizi mbili zina maana moja. Ayubu anatumia swali ili kukazi kwamba Mungu asingempa kitu kizuri kama angefanya dhambi na kuvunja ahadi yake.

Job 31:3

Maelezo ya jumla

Ayubu anaendelea kuzungumza

Je Mungu hazioni njia zangu na kuzihesabu hatua zangu zote?

Mahali hapa "njia zangu" na "hatua zangu" zinarejelea tabia za Ayubu. Ayubu anatumia swali kwa ajili ya mkazo.

Job 31:5

Maelezo ya jumla

Ayubu anaendelea kuzungumza

kama nime...

Katika 31:5-40 Ayubu anafafanua hali mbalimbali ambazo angesitahili kupata hukumu ya Mungu. Lakini anajua kuwa si ya kweli na yeye hana hatia.

nimetembea katika udanganyifu, kama mguu wangu umeharakisha katika uongo

"kufanya kitu cha uongo au kumdanganya mtu kwa makusudi"

na nipimwe katika vipimo vilivyo sawa

Watu hutumia mizani ili kupima vitu na kutambua uthamani wake. "Mungu na anihukumu kwa uadilifu"

Job 31:7

Maelezo ya jumla

Ayubu anaendelea kufafanua hali ambazo alistahili kupata hukumu ya Mungu, lakini anajua kuwa hayakuwa ni ya kweli.

Kama hatua zangu zimegeuka kutoka katika njia sahihi

"kama nimekoma kufanya kile kilicho sawa"

kama moyo wangu umetembea kwa kufuata macho yangu

"kama nimefanya mambo yoyote maovu"

na kama doa lolote la uchafu limeng'ang'ania katika mikono yangu

"kama nina hatia ya dhambi kabisa"

mavuno na yang'olewe katika shamba langu

"mtu mwingine zaidi na aje na kuchukua mavuno kutoka katika shamba langu"

Job 31:9

Maelezo ya jumla

Ayubu anaendelea kufafanua hali ambazo alistahili kupata hukumu ya Mungu, lakini anajua kuwa hayakuwa ni ya kweli.

kama moyo wangu umevutiwa na mwanamke mwingine

"kama nimemwakia tamaa mke wa mwanaume mwingine"

ikiwa nimelala na mke wa jirani yangu katika hali ya kusubiria katika mlango wake

"na kama nimemsubiria aache nyumba yake ili niweleze kulala naye"

na ndipo mke wangu na asage nafaka kwa mwanaume mwingine

Maana zinazokubalika ni 1) hii ni njia ya kusema kuwa mwanaume atalala na mke wa Ayubu au 2) in maana kwamba atakuwa mtumwa na kufanya kazi kwa mwanaume mwingine.

Job 31:11

Maelezo ya jumla

Ayubu anaendelea kufafanua hali ambazo alistahili kupata hukumu ya Mungu, lakini anajua kuwa hayakuwa ni ya kweli.

litakuwa ni kosa kubwa kuadhibiwa na waamuzi

"Litakuwa ni kosa ambalo kwa ajili yake waamuzi watakuwa sahihi kuniad

Kwa kuwa ni moto ambao unateketeza kila kitu kwa uharibifu, na kwamba utaunguza mavuno yangu yote

Ayubu anatia mkazo jinsi dhambi ya uzinzi iilivyo ya hatari na kuangamiza.

Job 31:13

Maelezo ya jumla

Ayubu anaendelea kufafanua hali ambazo alistahili kupata hukumu ya Mungu, lakini anajua kuwa hayakuwa ni ya kweli.

kisha nini basi ningefanya wakati Mungu anapoinuka ili kunishitaki mimi? Atakapokuja kunihukumu, nitamjibuje?

Ayubu anatumia swali ili kutia mkazo. "kisha hakutakuwa na kitu kabisa nitakachoweza kusema ili kujilinda mwenyewe wakati Mungu atakapokuja kunihukumu"

Je yeye aliyenifanya mimi tumboni hakuwafanya wao pia? Je yeye si yeye yule aliyetuumba sisi wote katika tumbo?

"Mungu, ambaye alinifanya mimi na kwa namna ile ile aliwafanya na wao, atanihukumu kwa jinsi ya haki ile ile kama anavyowahukumu wao."

Job 31:16

Maelezo ya jumla .

Ayubu anaanza kufafanua hali ambazo angestahili kupata hukumu ya Mungu, (zimeelezwa katika 31:22) lakini anajua kuwa hayakuwa ni ya kweli

nimesababisha macho ya wajane yafifie kwa kulia,

Mahali hapa "yafifie" inarejelea mjane kuwa wa uwezo mbaya wa kuona kwasababu ya kulia sana.

kipande changu

"chakula"

tangu ujana wangu yatima walikua pamoja nami kama kuwa na baba, nami nimemwongoza mama yake, mjane, tangu katika tumbo la mama yangu mwenyewe.

Ayubu anaelezea jinsi alivyowatendea kweli mjane na yatima. "Niliwajali yatima na wajane tantu nilipokuwa mdogo sana"

Job 31:19

Maelezo ya jumla .

Ayubu anaanza kufafanua hali ambazo angestahili kupata hukumu ya Mungu, (zimeelezwa katika 31:22) lakini anajua kuwa hayakuwa ni ya kweli

ikiwa moyo wake haujanibariki kwasababu amekuwa hajatiwa joto na sufu ya kondoo zangu,

"Nimewapa watu wale nguo za sufu ili kupata joto, na hivyo wamenibariki, lakini kama ningekuwa sijafanya hivyo,"

nimeinua juu mkono wangu kinyume

"Nimetisha ili kudhuru"

katika lango la mji

Hapa ni mahali ambapo watu muhimu wa mji hukusanyika na kufanya maamuzi.

Job 31:22

Maelezo ya jumla

Ayubu anaendelea kufafanua hali ambazo alistahili kupata hukumu ya Mungu, lakini anajua kuwa hayakuwa ni ya kweli.

Ndipo bega langu na lianguake kutoka katika sehemu yake, na mkono wangu uvunjike katika kiungo chake

"kisha mtu mmoja na alivunje bega langu na kuuvunja mkono wangu"

Job 31:24

Maelezo ya jumla

Ayubu anaendelea kufafanua hali ambazo alistahili kupata hukumu ya Mungu, lakini anajua kuwa hayakuwa ni ya kweli.

kama ningesema kwa dhahabu safi, 'wewe unanifanya kuwa na tumaini';

Msitari huu una maana sawa na msitari uliotangulia. Kwa pamoja inasisitiza kwamba Ayubu hajategemea mali ili kumletea usalama.

mkono wangu umepata mali nyingi,

"Nimepata mali nyingi kwa uwezo wangu"

Job 31:26

Maelezo ya jumla

Ayubu anaendelea kufafanua hali ambazo alistahili kupata hukumu ya Mungu, lakini anajua kuwa hayakuwa ni ya kweli.

mwezi ukitembea

"mwezi ukizunguka katika anga"

na kama moyo wangu umevutwa kwa siri

"kama kwa siri nimetamani kuviabudu"

mdomo wangu umeubusu mkono wangu

Hii ni ishara ya upendo na ibada.

kuadhibiwa na waamuzi,

"kwa ajili yake waamuzi wangekuwa sawa kuhukumu"

Job 31:29

Maelezo ya jumla

Ayubu anaendelea kufafanua hali ambazo alistahili kupata hukumu ya Mungu, lakini anajua kuwa hayakuwa ni ya kweli.

Kwa kweli sijauruhusu hata mdomo wangu kutenda dhambi kwa kuuomba uhai wake kwa laana.

Ayubu anaelezea ukweli wa jinsi alivyowatendea wale anaowachukia. "kwa ukweli, sikujihusisha mwenye katika dhambi kwa kuilaani sik yake"

Job 31:31

Maelezo ya jumla

Ayubu anaendelea kufafanua hali ambazo alistahili kupata hukumu ya Mungu, lakini anajua kuwa hayakuwa ni ya kweli.

Ikiwa watu wa hema yangu hawajasema,' Nani aweza kumpata mtu ambaye hayashibishwa na chakula cha Ayubu?

"Watu wangu siku zote wamekuwa na uwezo wa kusema,"Kila mtu tunayemjua amekula chakula kingi cha Ayubu kama alivyotaka' Kama hayo hayakuwa ya kweli,"

hata mgeni hajawahi kukaa katika pembe ya mji, kwa kuwa siku zote nimefungua milango yangu kwa ajili ya wasafiri

Ayubu anaelezea jinsi ambayo aliwatendea wageni."Wageni hawakuwahi kulala mitaani. Mara zote niliwakaribisha nyumbani kwangu"

Job 31:33

Maelezo ya jumla

Ayubu anaendelea kufafanua hali ambazo angestahili kupata hukumu ya Mungu, lakini anajua kuwa hayakuwa ni ya kweli.

kwa kuwa niliogopa kusanyiko kubwa, kwasababu ya matwezo ya familia yaliniogopesha

Kauli hizi zinamaanisha kitu kimoja. Kwa pamoja zinatia mkazo kwamba mtu anaweza kuificha dhambi yake kwasababu anahofu juu kile ambacho watu wangesema.

Job 31:35

hii ni saini yangu

Ayubu anaelezea malalamiko yake kwa Mungu kana kwamba aliyaandika katika nyaraka rasmi. Angeandika jina lake juu yake kama ahadi ambayo kila kitu katika nyaraka ni za kweli.

Ikiwa nilikuwa na shitaka rasmi ambalo adui yangu ameliandika!

"kama tu ningeweza kusoma mashitaka ya adui yangu dhidi yangu"

Hakika ningelibeba hadharani juu ya bega langu; ningeliweka juu kama taji

Hii ina maana kama Mungu angeyaandika mashitaka kinyume na Ayubu, kisha Ayubu angeziweka nyaraka mahali ambapo kila mtu angeweza kuzisoma.

hatua zangu

hii inarejelea matendo ya Ayubu

kama mwana wa mfalme mwenye kujiamini

Hii ina maana kwamba Ayubu angemkaribia Mungu bila hofu.

Job 31:38

Maelezo ya jumla

Hii inahitimisha maelezo ya Ayubu juu ya hali ambazo ndani yake angestahili hukumu ya Mungu, lakini anajua kuwa haikuwa kweli.

Kama nchi yangu ingelia dhidi yangu, na matuta yake yaomboleza pamoja

Ayubu anaielezea nchi kana kwamba alikuwa mtu ambaye analia kwasababu Ayubu ameiiba kutoka kwa mmliki halali.

Job 32

Job 32:1

katika macho yake mwenyewe

''katka ufahamu wake mwenyewe" au "katika mawazo yake"

Ndipo iliwaka hasira ya Elihu mwana wa Barakeli Mbuzi, wa familia ya Ramu, iliwaka dhidi ya Ayubu

Hii inalinganisha hasira ya Elihu na mtu anayewasha moto.

Elihu.....Barakeli.....Ramu

Haya ni majina ya wanaume

mbuzi

Hili ni jina la kikundi cha watu.

Job 32:3

Hasira ya Elihu iliwaka pia kinyume cha marafiki zake watatu

Hii inallingisha hasira ya Elihu na mtu anayewasha moto.

sasa

Neno hili limetumika hapa kuonesha pumziko fupi katika habari kuu. Hii inatueleza habari za nyuma kuha

uwa hapakuwa na jibu katika midomo ya watu hawa watatu

"kwamba watu hawa watatu walikuwa hawana kitu zaidi cha kusema"

hasira yake iliwaka

Hii tena inalinganisha hasira ya Elihu na mtu anayewasha moto. "alikuwa mwenye hasira sana"

Job 32:6

ninyi ni wazee

mahali hapa 'ninyi' ni wingi na inarejelea Ayubu na marafiki zake.

Urefu wa siku utazungumza; na wingi wa miaka utatufundisha hekima

Hii mistari miwili inamaanisha kitu kimoja. Elihu anatia mkazo kwa kuwa watu wazee ni wenye hekima kulika vijana, wanatakiwa kuwa wa kwanza kusema yale wanayoyajua.

Job 32:8

Maelezo ya jumla

Elihu anaendelea kuzungumza na Ayubu na marafiki zake.

roho.... pumzi ya Mwenye nguvu

Virai hivi vinamaanisha kitu kimoja. Elihu anakazia kwamba hekima ya watu hutoka kwa Mungu.

Job 32:11

niliyasubiria maneno yenu

Elihu anaongea na marafiki za Ayubu. "Nilisubiri nisikie yale ambayo mngesema"

Job 32:13

Maelezo ya jumla

Elihu anaendelea kuzungumza na marafiki zake na Ayubu.

Tumepata hekima

"sisi ni wenye hekima"

amemshinda Ayubu

"kumshawishi Ayubu" au "kumjibu Ayubu"

Job 32:15

Maelezo ya jumla

Elihu anaendelea kuzungumza

Hawa watu watatu wamep igwa bumbuwazi; hawawezi kuendelea kumjibu Ayubu; hawana neno zaidi la kusema

Vipande vitatu vya mstari hii vinamaanisha kitu kimoja. Elihu anakazia kwamba marafiki wa Ayubu wamesema kile walichoweza kusema.

Je ninapaswa kusubiria kwasababu hawazungumzi, kwa kuwa wamesimama pale kimya na wala hawajibu zaidi?

Elihu anatumia swali kukazia kwamba hatasubiria tena ili azungumze

Job 32:17

Maelezo ya jumla

Elihu anaendelea kuzungumza kwa kutumia mtindo wa usambamba

nimejawa na maneno

"nina mengi sana ya kusema"

roho ndani yangu inanisukuma

"lazima niseme sasa"

kifua changu ni kama divai yenye chachu ambayo haina tundu; kama viriba vipya, kiko tayari kupasuka.

Wakati divai inapochacha, gesi hujikusanya katika chombo. Kama gesi hiyo yaitaondolewa, chombo kitapasuka . Elihu anamaanisha kwamba anayo mengi ya kusema na kama hatayasema anajisikia kama atapasuka.

Job 32:20

Maelezo ya jumla

Elihu anaendelea kuzungumza kwa kutumia mtindo wa usambamba

niweze kuburudishwa

"naweza kujisikia vizuri"

nitafungua kimya changu

"fungua mdomo wako"au "sema"

wala sitatoa sifa za majina kwa mtu yeyote

"wala sitamsifu mtu yeyote au kumpa mtu majina ya heshima"

Muumba wangu

"Mungu aliyeniumba"

Job 33

Job 33:1

Maelezo ya jumla

Elihu anaendelea kuzungumza

usikilize hotuba yangu; sikiliza maneno yangu yote

Virai hivi viwili vinamaanisha kitu kimoja. Elihu anatia mkazo kwamba Ayubu lazima asikilize kwa makini.

nimeufumbua mdomo wangu; ulimi wangu umesema maneno ndani ya mdomo wangu

Kauli hizi zinamaanisha kitu kimoja. Elihu anatiza mkazo kwamba sasa ana utayari wa kuzungumza.

Maneno yangu yatasema uadilifu wa moyo wangu

"Nitazungumza kwa ukamilifu wa uadilifu"

yatasema kwa unyofu yale ambayo mdomo wangu unayajua.

"Nitakwambia kwa uaminifu mambo ninayoyajua"

Job 33:4

Maelezo ya jumla

Elihu anaendelea kuzungumza na Ayubu

Roho ya Mungu imeniumba..... imenipatia uhai

mistari hii miwili ina maana moja. Elihu inatia mkazo kwamba Mungu amemfanya yeye na kwa hivyo humpa mamlaka kwa kile anachokisema.

weka maneno yako katika mpangilio mbele yangu na kisha usimame

"andaa kile utakachokisema na unijibu"

Job 33:6

Maelezo ya jumla

Elihu anaendelea kuongea na Ayubu.

nimeumbwa pia kutoka katika udongo

"Mungu amenifanya kutokana na udongo"

wala mzigo wangu hautakuwa mzito kwako.

"Sitakutesa wewe kwa kile ninachokisema" au " nitazungumza na wewe kwa upole"

Job 33:8

Maelezo ya jumla

Elihu anaendelea kuongea na Ayubu

nimeisikia sauti ya maneno yako yakisema

"Nimekusikia ukisema"

'Mimi ni safi na bila hila; sina hatia, na hakuna dhambi ndani yangu.

Maelezo yote haya yanamaanisha kitu kile kile. "Mimi sina hatia ya kosa lolote"

Job 33:10

Elihu anaendelea kunukuru kile alichomsikia Ayubu akikisema

"akiba" ni vizuizi ya mbao ambayo ilitumika na bwana jela ambaye aliiweka katika miguu ya wafungwa kuwazuia wasitoke.

njia zangu

Hii inarejelea matendo ya Ayubu

nitakujibu

Elihu anazungumza na Ayubu

Job 33:13

Maelezo ya jumla

Elihu anaendelea kuzungumza na Ayubu

Kwanini unashindana naye?

"hatutakiwi hata kujaribu kushindana na Mungu"

Huwa hahesabu matendo yake yoyote.

"Yeye hawajibiki kutueleza sisi kila kitu anachokifanya"

Mungu huzungumza mara moja, naam, mara mbili,

"Mungu huzungumza tena na tena kwa njia mbalimbali

Katika ndoto, katika maono ya usiku,

Maneno haya yanamaanisha kitu kile kile. "ndoto ambayo katika maono ya usiku"

wakati usingizi mzito unapowapata watu, katika usingizi kitandani

"wakati watu wakiwa wamesinzia kweli kitandani mwao"

Job 33:16

Maelezo ya jumla

Elihu anaendelea kuzungumza na Ayubu

Mungu hufungua masikio ya watu

"ndipo Mungu hufunua mambo kwa watu"

Mungu huyaokoa maisha ya mwanadamu kutoka katika shimo, na uhai wake dhidi ya kifo.

Maelezo ya haya yanamaanisha kitu kile kile. "Mungu huwakoa watu kutoka katika kaburi na katika kifo."

Job 33:19

Maelezo ya jumla

Elihu anaendelea kuongea na Ayubu

Mtu huadhidibiwa pia

"Mungu pia humwadhibu mtu"

ili kwamba maisha yake yachukie chakula, na roho yake ichukie vyakula vizuri

Virai hivi viwili kimsingi vinamaanisha kitu kile kile, kwamba mtu ni yuko katika maumivu makali ambayo yanamfanya anashindwa hata kula.

ichukie vyakula vizuri

"kuchukia hata chakula chake anachokipendelea"

Job 33:21

Maelezo ya jumla

Elihu anaendelea kuzungumza na Ayubu

Nyama yake imeharibiwa ili kwamba usionekane; mifupa yake

"Ugonjwa huufanya mwili wake uwe dhaifu na ukonde hata kwamba mtu anaweza hata kuona mifupa yake"

roho yake inasogea shimoni

"yuko karibu kuingia katika kaburini"

uhai wake unasogea kwa wale wanaotaka kuuharibu.

Kirai "wale wanaotaka kuuharibu" yaweza kurejelea watu wale ambao wako tayari katika sehemu ambapo wafu huenda. Yaweza pia kurejelea malaika wa kifo ambaye huja na kumfanya mtu afe. "Yuko karibu na kufa"

Job 33:23

Maelezo ya jumla

Elihu anaendelea kuongea na Ayubu

kwa ajili yake

Hii haimrejelei mtu maalumu. Elihu anaendelea kuongea na mtu yeyote kwa ujumla.

mmoja miongoni mwa maelfu ya malaika,

"mmoja kutoka katika kundi kubwa la malaika"

Job 33:25

Maelezo ya jumla

Elihu anaendelea kuongea na Ayubu

kisha

"kama matokeo ya ombi la malaika kwa Mungu"

mwili wake utakuwa mororo kuliko mwili wa mtoto

"mwili wa mtu mgonjwa utakuwa mpya tena kama mwili wa mtu mdogo"

atazirudia siku za nguvu za ujana wake.

"atakuwa na nguvu tena"

auone uso wa Mungu akiwa mwenye furaha

"humwabudu Mungu kwa furaha"

Mungu atampa mtu ushindi wak

"Mungu atamwokoa mtu" au "Mungu atayafanya mambo ya mtu kuwa sawa" Hii pia yaweza kumaanisha kwamba mtu anatangaza kwa wengine jinsi Mungu alivyomwokoa.

Job 33:27

Maelezo ya jumla

Elihu anazidi kuzungumza na Ayubu

lakini dhambi yangu haikuadhibiwa

"lakini Mungu hakuniadhibu mimi kwa kutenda dhambi"

ameiokoa roho yangu

"aliniokoa mimi"

maisha yangu yataendelea kuuona mwanga

Atauona mwanga wa maisha badala ya giza ambalo angeliliona katika kifo. "nitaendelea kuishi"

Job 33:29

Maelezo ya jumla

Elihu anazidi kuzungumza na Ayubu

mara mbili, naam, hata mara tatu

"tena na tena"

roho yake

:yeye"

aweze kumlikwa na mwanga wa maisha.

"aweza kuwa na furaha ya kubaki kuwa hai"

Job 33:31

Maelezo ya jumla

Elihu anazidi kuongea na Ayubu

zingatia na unisikilize mimi;

Virai hivi vinamaanisha kitu kile kile. "Nisikilize kwa umakini, Ayubu"

Job 34

Job 34:1

Elihu

Angalia jinsi alivyofasiri katika 32:1

Sikilizeni maneno yangu

"Sikiliza kile ninachokisema"

ninyi watu wenye hekima....ninyi mlio na maarifa

Elihu anamkosoa Ayubu na marafiki zake. Hafikiri kama ni watu wenye hekima kweli.

Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama ambavyo kaakaa huonja chakula.

Elihu anamaanisha kwamba watu wasikilize kwa makini ili kujua kilicho cha haki au kibaya kama tu vile ambavyo tunaonja chakula kutambua kama ni chakula kizuri au kibaya.

Job 34:4

Maelezo ya jumla

Elihu anazidi kuongea

Na tujichagulie sisi

Hapa "sisi" inamrejelea Elihu, Ayubu, na marafiki wake watatu.

ameondoa haki zangu

"amekataa kunipa haki "

, ninaangaliwa kama mwongo

"marafiki zangu hudhani mimi ni mwongo" Hii huenda yaweza kumaanisha: "Mungu hasemi ukweli kuhusu mimi"

Kidonda changu hakiponyeki,

"mimi ni mgonjwa na hakuna awezaye kuniponya"

Job 34:7

Maelezo ya jumla

Elihu anazidi kuzungumza

Ni mtu gani aliye kama Ayubu

Elihu anatumia swali hili kumkaripia Ayubu. " Hakuna mwingine zaidi kama Ayubu"

ambaye hunywa dharau kama maji

Elihu anamshitaki Ayubu kwa kufurahia kuwadharau watu wengine.

ambaye hutembea pamoja na watu waovu

"ambaye anaenenda kama watu waovu"

Job 34:10

Maelezo ya jumla

Elihu anazidi kuongea

enyi watu wenye ufahamu

Elihu anamkosoa Ayubu na marafiki zake. Hadhani kabisa kama walikuwa ni watu wenye hekima.

iwe mbali na Mwenye enzi kwamba atatenda dhambi

Hii ina maana sawa na sehemu nyingine ya sentensi iliyotangulia. Elihu anakazia kwamba Mungu siku zote hufanya yaliyo ya haki.

humfanya mtu apate thawabu za njia zake mwenyewe

Hii inamaana sawa na sehemu nyingine ya sentensi iliyotangulia. Elihu anatia mkazo kwamba Mungu huwapa watu kile wanachostahili.

Mungu hatendi uovu, wala Mwenye nguvu hajaIpotosha haki.

Hii ina maana sawa na sehemu nyingine ya sentensi iliyotangulia. Elihu anakazia kwamba Mungu siku zote hufanya yaliyo ya haki.

Job 34:13

Maelezo ya jumla

Elihu anaendelea kuzungumza

Ni nani aliyemweka kuwa mtawala wa dunia? Ni nani aliyeiweka dunia yote chini yake?

Kauli hii ina maana moja. "hakuna hata mmoja ambaye anahitaji kumpa Mungu ruhusa ili anaye majukumu yake juu ya dunia yote. Yeye ni mwenye haki katika kuutawala ulimwengu wote."

nafsi yake na pumzi yake

"nafsi yake na pumzi amabayo hutupa uzima"

miili yote

"viumbe hai vyote "

Job 34:16

Maelezo ya jumla

Elihu anaendelea kuzungumza

sasa

Elihu anatumia neno hili ili kuleta usikivu wa kitu fulani muhimu ambacho alikuwa karibu kukisema.

sikilizeni sauti ya maneno yangu

Hii ina ina maana ile ile na ya sehemu iliyotangulia ya sentensi. "sikiliza kile ninachosema"

Je yeye anayeichukia haki aweza kutawala? Je mtamhukumu Mungu kuwa ni mwenye makosa, ambaye ni mwenye haki na mwenye nguvu?

"Yeye anayechukia haki hawezi kutegemea kuwa kiongozi juu

Job 34:18

Maelezo ya jumla

Elihu anaendelea kuzungumza

Mungu ambaye humwambia mfalme, ' Wewe ni mbaya; au huwaambia wenye kuheshimiwa, 'Ninyi ni waovu'?

Hii inaendeleza swali kutoka katika mstari uliotangulia.

mbaya

"mwovu" au "asiyestahili"

, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake

Mahali hapa neno "mkono" linamaanisha nguvu.

wakati wa usiku watu watatikiswa na watapita

"wakati wa usiku" ni wakati wa mwisho wa siku na mwanzo wa siku nyingine.

watu wenye nguvu watatwaliwa mbali,lakini si kwa mikono ya wanadamu.

"Ni Mungu wala si wanadamu anayewafanya watu wa muhimu wafe.

Job 34:21

Kwa kuwa macho ya Mungu yako juu ya njia za mtu;

"kwa kuwa Mungu huangalia kila kitu anakifanyacho mtu

anaziona hatua zake zote

"humwona kila aendako"

Hakuna giza, wala hakuna weusi mzito

Maneno "weusi mzito" kimsingi yanamaanisha kitu kile kile na yanatia uzito juu ya neno "giza"

Job 34:24

Maelezo ya jumla

Elihu anaendelea kuzungumza

Huwavunja vipande vipande watu wenye nguvu

"Huwaharibu watawala"

kwa ajili ya njia zao ambazo hazihitaji uchunguzi zaidi

"kwasababu anajua tayari kile alichokifanya"

huwaweka watu wengine katika nafasi zao

"na anachagua watu wengine kutawala katika nafasi zao"

wakati wa usiku

"wakati wasioutarajia"

Job 34:26

Maelezo ya jumla

Elihu anaendelea kuzungumza

dhahiri mbele za watu wengine

"katika sehemu ambayo kila mtu anaweza kuona"

wamegeuka na kuacha kumfuata yeye

"wangeacha kumtii yeye"

njia zake

Hii inarejelea maagizo ya Mungu kwa jinsi ambavyo watu wanapaswa kuenenda.

wamekifanya kilio cha watu masikini kimfikie

"waliwafanya watu masikini walie, na Mungu aliwasikia"

Job 34:29

Maelezo ya jumla

Elihu anaendelea kuzungumza

Na wakati akaapo kimya, nani aweza kumhukumu kuwa mkosaji?

Elihu anatumia swali kwa ajili ya kumfundisha Ayubu. "Hakuna anayeweza kumkosoa Mungu kama akiamua kukaa kimya"

Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumjua?

Elihu anatumia swali jingine kwa sababu ile ile. "Hakuna hata mmoja anayeweza kwenda na kumwona kama akiamua kujificha mwenyewe."

asiwepo mtu wa kuwanasa watu.

Hii inawalinganisha watu watawaua na muwindaji ambaye hunasa nyara zake.

Job 34:31

Maelezo ya jumla

Elihu anaendelea kuzungumza

nifunze kile ambacho siwezi kukiona

"nifundishe kile nilichokifanya vibaya na hata sikukijua"

Je unadhani kwamba Mungu ataiadhibu dhambi ya mtu huyo, kwa kuwa unayachukia yale ambayo Mungu huyatenda?

Elihu anatumia swali kwa ajili ya kutia mkazo. "Ingawa haupendi kile ambacho Mungu anakifanya, hakika hata haufikirii kwamba Mungu atamwadhibu mtu huyu"

Job 34:34

Maelezo ya jumla

Elihu anaendelea kuzungumza

Job 34:36

Kama Ayubu alijaribiwa kwa kitu kidogo kabisa katika kesi yake

"kama tu tungeweza kumpeleka Ayubu mahakamani ili kwamba hakimu aweze kumsikia kwa malalamiko yake yote."

anapiga makofi ya dharau kati yetu

"Humdharau Mungu mbele yetu hasa"

anaweka maneno kinyume na Mungu

"anaendelea kusema mambo mabaya kumhusu Mungu"

Job 35

Job 35:1

Je unadhani hii ni sawa ....'Haki yangu mbele ya Mungu?

Elihu anatumia maswali ili kumtia changamoto Ayubu. "Lazima ufikiri wewe ni mwenye haki....haki yangu mbele za Mungu"

Je unadhani

hapa kiambishi 'u' ni umoja na kinamwakilisha Ayubu.

Kwa kuwa unauliza, 'Inafaa nini kwangu' na 'Ingekuwa nzuri kwangu kama ningekuwa nimetenda dhambi?

"kwa kuwa wasema haijalishi kuwa uko mwenye haki, na ya kwamba hakuna faida zaidi kwako kuliko kama ungekuwa umetenda dhambi"

Job 35:4

Maelezo ya jumla

Elihu anaendelea kuzungumza

Job 35:6

Sentensi kiunganishi

Elihu anaendelea kuongea

Kama umetenda dhambi, ni madhara gani huwa unayafanya kwa Mungu?

Dhambi zako zote haziwezi kumharibu mtu au tabia za Mungu"

Ikiwa makosa yako yameongezeka zaidi, je huwa unafanya nini kwake?

Swali hili linarudia wazo lile lile kama swali lililotangulia. "Ingawa unaendelea kutenda dhambi pamoja na matokeo makubwa, dhambi zako hazina athari juu yake.

Kama wewe ni mwenye haki, unaweza kumpa nini? Je atapokea nini mkononi mwako?

Maswali haya mawili kimsingi yanamaanisha jambo lile lile, kwamba haki ya Ayubu haikuongeza chochote kwa Mungu.

kutoka mkononi mwako

"kutoka kwako"

mwana wa mtu

"mwanadamu mwenza" au "mtu mwingine"

Job 35:9

Maelezo ya jumla

Elihu anaendelea kuzungumza

katika mikono ya watu wenye nguvu

Mahali hapa "mikono" ina maana ya ya nguvu au uwezo.

Lakini hakuna hata mmoja asemaye, ' Mungu Muumba wangu yuko wapi....ndege wa angani?

"Lakini mtu wa haki kweli si mwenye kiburi hata kwa kusema kwamba Mungu amekataa kuwapa uwezo wa kuimba nyimbo za furaha, wakati wa mateso yao."

ambaye hutoa nyimbo wakati wa usiku,

Hii ina maana kwamba ahadi za Mungu huwapa watu sababu ya kuwa na furaha hata wakati wakiwa katika mateso.

Job 35:12

Maelezo ya jumla

Elihu anaendelea kuzungumza

wanalia

" watu walioteswa wanalia"

Ni kwa namna gani atakujibu

"Hakika hatakujibu"

Job 35:15

Maelezo ya jumla

Elihu anaendelea kuzungumza

Ni kwa jinsi gani atakujibu

"Hakika hatakujibu"

huongeza maneno

"anaendelea kuongea"

Job 36

Job 36:4

maneno yangu hayatakuwa ya uongo;

"Nitasema yale ya kweli"

angalia

Neno 'angalia' mahali hapa linatia mkazo juu ya kile kinachofuata. "hakika"

yeye ni mwenye nguvu katika uweza wa ufahamu

Kirai "mwenye nguvu katika uweza" kina maana "kuwa na nguvu zaidi"

Job 36:6

Haondoi macho yake kwa wenye haki

"huwaangalia wale wenye haki"

huwaweka juu ya viti vya enzi kama wafalme

Yahweh huwaheshimu watu kama watu wanavyowaheshimu wafalme.

nao wameinuliwa juu

Maana zinazokubalika ni 1) anawafanya wengine" au 2)"anawafanya wengine wafanikiwe"

Job 36:8

wamefungwa minyororo

Hapa kiambishi 'wa' kinawarejelea watu kwa ujumla. "mtu mmoja aliwafunga kwa minyororo''

kunaswa katika kamba za mateso

Elihu anaongelea juu ya mateso kana kwamba yanaweza kuwanasa watu kwa kamba. "kama mtu atawafanya wateseke"

Job 36:10

Hufungua pia masikio yao kwa ajili ya agizo lake

"huwafanya wasikilize agizo lake"

siku zao....miaka yao

Virai hivi viwili rinarejelea kipindi cha maisha ya mtu.

wataangamia kwa upanga

"watakufa kifo cha vurugu"

Job 36:13

Na wale wasiomjua Mungu hutunza hasiria zao katika mioyo

Mahali hapa neno "moyo" linarejelea "fikra na hisia"

Job 36:15

hufungua masikio yao

angalia ulivyotafsiria katika 36:10

meza yenu ingewekwa

"Watumishi wako wangeiweka meza yako"

chakula kilichojaa mafuta

nyama yenye mafuta mengi ilikuwa ni ishara ya mafanikio kwasababu wanyama walikuwa na afya njema na walilishwa vizuri. "vyakula vizuri sana"

Job 36:17

wewe umejaa hukumu juu ya watu waovu

Maana zinazokubalika ni 1)" Mungu anakuhukumu kama ambavyo angewahukumu watu waovu" au 2) "umejawa na kushikwa na hukumu ambayo watu waovu wanastahili"

hukumu na haki umeziachilia

"Mungu amekuleta katika hukumu na amekupa haki"

Usiuache utajiri ukuvute katika udanganyifu;

Usimruhusu mtu akuvute katika udanganyifu kwa mali.

sehemu kubwa ya rushwa isikugeuze upande kutoka katika haki.

"Usimruhusu mtu akugeuze upande kutoka katika haki kwa rusha kubwa.

Job 36:19

Je utajiri wako waweza kukunufaisha, ili kwamba usiwe katika taabu, au nguvu zako zote za uwezo zaweza kukusaidia?

Elihu anauliza maswali haya ili kutia mkazo kwamba pesa na nguvu hazitaweza kumsaidia Ayubu kama atatenda isivyo haki.

nguvu zako zote za uwezo

"nguvu zako zote kubwa"

wakati ambapo mataifa hukatiliwa mbali katika nafasi zao

Maana zinazokubalika ni 1)" wakati makundi ya watu yatakapotoweka kutoka katika sehemu yake au 2) " wakati watu watakapowavuta kutoka katika nyumba zao,"

unajaribiwa kwa mateso

"Mungu anakujaribu wewe kwa kukufanya uteseke"

Job 36:22

Angalia

Neno 'angalia' mahali hapa linaongeza mkazo kwa kile kinachofuata

nani aliye mwalimu kama yeye?

Jibu lililofichwa kwa swali hili ni "hakuna" "Hakuna mwalimu kama yeye" au "hakuna awezaye kufundisha kama anavyofanya yeye"

Ni nani alishamwalekeza njia yake?

"Hakuna hata mmoja ambaye alishamwamuru yeye na kumwelekeza kitu cha kufanya.

Job 36:25

kwa mbali

""Isiyo kamili"

Tazama

Neno "tazama" mahalip hapa linaongeza kile kijacho.

hesabu ya miaka yake

"umri wake"

Job 36:27

kuna hata mmoja awezaye kuelewa kwa undani kusambaa kwa mawingu na radi kutoka katika nyumba yake?

Jibu lisilo la wazi ni "Hapana"

nyumba yake

Mahali hapa ni "nyumba yake" inawakilisha anga la juu mahali ambapo Mungu hudhani kuwa huiishi huko.

Job 36:30

Angalia

Neno 'angalia' mahali hapa linaongeza mkazo kwa kile kinachofuata.

Job 36:32

Yeye huuijaza mikono yake kwa mwanga

Maana zinazokubalika ni 1) kwamba Mungu anashikilia vifungo vya mwanga mkononi mwake ili aweze kuzitupa au 2) kwamba Mungu huuficha vifungo vya mwanga katika mikono yake hadi pale alipo tayari kuvitumia.

ngurumo zake

"Sauti ya mwangaza"

Job 37

Job 37:1

moyo wangu hutetemeka...umeondolewa kutoka katika sehemu yake

Virai hivi viwili kimsingi vina maana moja ile ile na kutia mkazo wa ukubwa wa hofu yake.

moyo wangu hutetemeka kwa hili

Neno 'hili' linarejelea dhoruba katika 36:32

umeondolewa kutoka katika sehemu yake

Mapigo ya moyo wa Elihu yanaongelewa kana kwamba yalikuwa yanaruka nje ya kifua chake.

kelele za sauti yake, sauti inayotoka katika mdomo wake.

Virai hivi viwili kimsingi vina maana ile ile. Elihu anaiongelea sauti ya radi kana kwamba ni sauti ya Mungu.

mipaka ya dunia

"sehemu yeyote katika dunia"

Job 37:4

Sauti huunguruma baada yake...mshindo wa mwanga wakati sauti yake inaposikika

Elihu anaendelea kuzungumzia radi kana kwamba ni sauti ya Mungu.

wakati sauti yake inaposikika

"wakati watu wanapoisikia sauti yake"

Job 37:7

Huuzuia mkono wa kila mtu

"humzuia kila mtu"

Dhoruba hutoka katika chumba chake upande wa kusini na baridi kutoka katika pepo zilizotawanyika katika upande wa Kaskazini.

Katika Israeli, upepo mkali wa dhoruba huvuma kutoka kusini na hewa ya baribi hufika kutoka kaskazini.

chumba chake upande wa kusini

Elihu anaongelea dhoruba kuwa ina sehemu inapokaa mpaka

Job 37:10

Barafu imetolewa kwa pumzi ya Mungu

Elihu anaongelea juu ya upepo wa baridi wa kaskazini kana kwamba ni pumzi ya Mungu. "Pumzi ya Mungu hufanya barafu"

umeganda kama chuma

wakati maji yanapoganda, huwa magumu kama chuma

Job 37:14

Je unajua ni kwa namna gani Mungu hushurutisha mawingu na kuufanya mwanga wa radi ung'ae ndani yake?

Jibu lililojificha la swali hili ni ''hapana''.

Job 37:16

Je unafahamu kuelea kwa mawingu, matendo ya ajabu ya Mungu, Je ni nani aliyemkamilifu katika maarifa?

"Haufahamu kuelea kwa mawingu, matendo ya ajabu ya Mungu, ambaye ni mkamilifu katika maarifa."

kuelea kwa mawingu

"jinsi mawingu yanavyoelea"

matendo ya ajabu ya Mungu

"njia za miujiza ambayo kwayo huyafanya mawingu yaelee katika anga"

Je unafahamu ni kwa jinsi gani mavazi yako huwa ya moto wakati nchi ikiwa imetulia kwasababu ya upepo unaotoka upande wa kusini?

"Wewe haufahamu jinsi ya kuzuia kutoka kwa jasho katika nguo zako; ni hatari sana wakati upepo wa joto kali unapokoma kuvuma kutoka kusini na majani yote katika miti hutulia"

Job 37:18

Je unaweza kulitandaza anga kama anavyofanya - anga ambalo lina nguvu kama kioo cha chuma kigumu?

"Hauwezi kulitandaza anga kama anavyoweza kwa anga ambalo ni gumu kama kioo cha chuma kigumu"

nguvu kama kioo cha chuma

Katika siku za Biblia, vioo vilitengenezwa kwa chuma. Elihu anaongelea anga kama anavyoangalia chuma kigumu wakati halitoi mvua.

chuma kigumu

Hii inarejelea chuma kilichoyeyushwa, na kumwagwa

Tufundishe sisi kile tunachopaswa kumwambia yeye

'mahali hapa maneno 'sisi' na kiambishi 'tu' yanamrejelea Elihu, Elifazi, Bildadi na Zofari, lakini si Ayubu. Elihu anatumia kirai hiki kwa kejeli.

kwasababu ya kiza katika akili zetu.

"kwasababu hatufahamu"

je anapaswa kuambiwa kwamba ninapenda kuongea naye?

"Sitakuwa na mtu wa kumwambia kwamba ninataka kuongea naye"

Je anapaswa kuambiwa

"je nipate mtu wa kumwambia"

Je mtu angependa kumezwa?

"Hakuna mtu ambaye angependwa kumezwa"

kumezwa

"kwa ajili ya Mungu kumwua"

Job 37:23

wale ambao ni wenye hekima katika akili zao wenyewe.

"wale wanaojidhania kuwa ni wenye hekima"

Job 38

Job 38:1

"Huyu ni nani ...... bila maarifa?

Yahweh anatumia swali hili ili kutia mkazo kwamba Ayubu alikuwa ameseam mambo ya kipumbavu. "Umeleta giza.... pasipo ufahamu."

aletaye giza katika mipango

Giza linawakilisha ushari wa kipumbavu.

kwa njia ya maneno bila maarifa?

"kwa kusema maneno lakini pasipokuwa na maarifa"

jifunge kiunoni mwako

"jifunge nguo yako kiuoni" Wanaume wajifunga nguo kuzunguka viunoni mwao, ili kwamba miguu iwe huru katika vita au mashindano.

kama mwanaume

"Kama shujaa"

lazima unijibu

"lazima animbie majibu"

Job 38:4

Maelezo ya jumla

Yahweh anaendelea kumtia changamoto Ayubu.

Wewe ulikuwa wapi... misingi

Yahweh anaumia swali hili il kutia mkazo kwamba Ayubu hakuwepo wakati Mungu alipoumba dunia, hivyo Ayubu haelewi jinsi Mungu alivyoiumba dunia.

ilipoitandaza misingi ya dunia

"Nilifanya misingi ya dunia" Yahweh anaelezea jinsi alivyoiumba dunia kana kwamba alikuwa akijenga jengo.

Niambie

"Niambie jibu"

kama unao ufahamu zaidi

"unadhani unajua sana"

ni nani aliyeamuru vipimo vyake

Yahweh anatumia swali hili kutia mkazo kwamba ni yeye anayeamua namna ukubwa wa dunia unavyopaswa kuwa, hivyo ni yeye pekee anayejua jinsi alivyoifanya.

alivinyosha vipimo juu yake

"aliipima dunia kwa kamba"

kipimo

kamba ambayo watu waliitumia ili kuhakiki kuwa wanajenga jengo kwa kipimo halisi na kwa muundo sahihi.

Job 38:6

Maelezo ya jumla

Yahweh anaendelea kumtia changamoto Ayubu

Ni nani............jiwe la pembeni

Yahweh anatumia maswali haya kutia makazo kwamba Ayubu hajui jinsi Yahweh alivyoifanya dunia.

Misingi yake ilitandazwa juu ya nini?

Ni juu ya nini misingi ya dunia iliwekwa.

nyota za asubuhi

"nyota angavu ambazo huangaza asubuhi"

wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja

Yahweh anaelezea juu ya nyota kana kwamba walikuwa ni watu walioweza kuimba.

wana wa Mungu

"malaika"

kwa furaha

"kwasababu walikuwa na furaha imejaa"

Job 38:8

Maelezo ya jumla

Yahweh anaendelea kumtia changamoto Ayubu.

huifunga bahari

Yahweh anatumia swali hili ili kutia mkazo kwamba aliifanya bahari.

huifunga bahari kwa milango

Yahweh analinganisha njia aliyoitumia kuizuia bahari ili isiigharikishe dunia yote na kuishikilia bahari kwa nyuma.

kana kwamba inatoka katika tumbo

Yahweh analinganisha uumbaji wake wa bahari na uzazi.

mavazi yake

kama nguo kwa ajili ya bahari

giza nene

:mawingu meusi sana"

na giza nene kuwa mkanda wake wa kujifungia

"na kufunga katika mawingu mazito Kama mkanda wa kujifungia"

mkanda wake wa kujifungia

Hiki ni kipande cha nguo ambacho watu walikitumia kuwafunga watoto wachanga baada ya kuzaliwa.

Job 38:10

Maelezo ya jumla

Yahweh anaendelea kumtia changamoto Ayubu

apo ilikuwa wakati nilipoweka bahari mpaka wangu,

Nlifanya mipaka kwa ajili ya bahari.

mpaka

Yahweh aliumba mpka kuzunguka bahari kwamba bahari haziruhusiwi kuuvuka.

nilipoweka makomeo yake na milango,

Yahweh analinganisha namna alivyotengeneza mpaka wa bahari na ya kwamba bahari ina milango na makomeo. "Hivyo niliweka vizuizi ili kwamba maji yasiweze kuvuka juu ya nchi."

makomeo

ni kpande kirefu cha ubao au chuma ambacho hutumika kwa ajili ya kufungia mlango.

kwa fahari ya mawimbi yako

Yahweh anazungumzia juu ya mawimbi kana kwamba walikuwa ni watu. Ina maana kwamba mawimbi yana fahari kwa kuwa yana nguvu.

Job 38:12

Maelezo ya jumla

Yahweh aendelea kumtia changamoto Ayubu.

Je tangu mwanzo wa siku zako, ulishawahi .....waovu watikiswe mbali nayo?

Yahweh anatumia swali hili kutilia mkazo kwamba ni Mungu tu anazo nguvu juu ya asubuhu na Ayubu hana hizo nguvu.

tangu mwanzo wa siku zako

Kirai hiki kina maana "tangu ulipozaliwa" au "katika siku

kuigiza asubuhi

Yahweh anaeilezea asubuhi kana kwamba alikuwa ni mtu ambaye angeweze kupokea maagizo.

a kuyafanya mapambazuko yajue sehemu yake katika mpangilio wa vitu

"uyaache mapambazuko yajue kule miliki yake iliko"

mapambazuko

ni mwanga unajitokeza asubuhi kabla ya jua halijachomoza.

ili kwamba ishikilie sehemu za dunia

Yahweh anaiongelea asubuhi kana kwamba ni mtu anayeshikila pembe za dunia kama pembe za mkeka. Mapambazuko yanaonekana kushikilia sehemu za dunia kwasababu mwanga wake huonekana kwanza pembezoni.

ili watu waovu watikiswe mbali nayo.

''na kuwatikisa watu waovu nje ya dunia." Mwanga wa mapambazuko huwafanya watu waovu waende mbali kama kutikisa kwa mkeka kunavyotoa uchafu juu yake.

Job 38:14

Dunia imebadilishwa katika mwonekano kama udongo unavyobadilika chini ya muhuri;

Watu hawawezi kuona vizuri kwa wakati wa usiku, lakini asubuhi hufunua wazi muundo wa kila kitu, kama vile muhuri unavyoumba mwonekano katika udongo.

Mwanga' wao umeondolewa kutoka kwa watu waovu

"Asubuhi huondolea mbali mwanga wa watu waovu"

mwanga wao

Watu waovu hudhani giza kuwa ndio mwanga wao, kwa kuwa wanafanya matendo yao maovu katika giza na wameizoelea giza.

mkono wao ulioinuliwa umevunjwa

Mkono ulioinuliwa wa watu waovu unaonesha kwamba wana nguvu na nia ya kufanya mambo maovu, lakini mwanga wa asubuhi huvunja mkono wa ili kwamba wasiwe na uwezo wa kufanya maovu.

Job 38:16

Maelezo ya jumla

Yahweh aendelea kumtia changamoto Ayubu.

Je ume...upana wake?

Yahweh anatumia maswali haya ili kutia mkazo kwamba vitu hivi ambavyo Ayubu hajavifanya na ya kwamba kuna vitu vingi sana ambavyo Ayubu havijui.

vyanzo

"chemichemi"

kilindi

"maji"j au "bahari" au "vilindi vya maji"

Je malango ya mauti yamefunuliwa kwako?

"Je kuna mtu amekuonesha malango ya kuzimu"

e umeifahamu dunia katika upana wake?

"Je umekiangalia kila kitu kkwa umakini katika njia zake kwa sehemu za mbali sana za dunia"

kama unayajua yote hayo

"kama umezoea dunia yote" au "kama unajua kila kitu kuhusu dunia"

Job 38:19

Maelezo ya jumla

Yahweh aendelea kumtia changamoto Ayubu.

sehemu ya kupumzikia kwa mwanga,

"sehemu ambayo mwanga hukaa" au " sehemu ambayo mwanga unaishi" Yahweh anauelezea mwanga kana kwamba alikuwa ni mtu.

sehemu zake za kazi

"kwa mpaka wake' Mpaka huizunguka sehemu ya mwanga na giza. Wakati usiku unapoisha, giza hurudi katika sehemu yake. Na wakati siku inapoisha, mwanga hurudi katika sehemu yake.

Bila shaka......kubwa sana!

Yahweh anatumia kejeli ya kinyume ili kutia mkazo kwamba Ayubu hauelewi mwanga na giza. "Ni wazi kwamba hauelewi kwa sababu ulikuwa bado haujazaliwa wakati nilipoviumba na haukuwa mtu mzima"

kwa kuwa ulizaliwa wakati huo

Neno 'wakati" linarejelea muda ambao mwanga uliumbwa na kutengwa na giza. "kwa kuwa ulikuwa umezaliwa wakati nilipouumba ulimwengu"

hesabu ya siku zako ni kubwa sana!

"umeishi miaka mingi sana ' au wewe ni mzee sana"

Job 38:22

Maelezo ya jumla

Yahweh anaendelea kumtia changamoto Ayubu

ume....juu ya dunia?

Yahweh anatumea maswali haya kukazia kwamba Ayubu hajui jinsi ambavyo Yahweh hutuma barafu, mawe ya mvua, radi na upepo wa mashariki juu ya nchi.

mawe ya mvua

vipande vya mviringo vya barafu ambavyo huanguka ardhini kutoka angani.

Job 38:25

Maelezo ya jumla

Yahweh anaendelea kumtia changamoto Ayubu.

Ni nani aliyezitengeneza mifereji

Yahweh anatumia swali hili kutia mkazo kwamba yeye ndiye hufanya mambo haya yote.

gharika ya mvua

"mbubujiko wa nguvy wa mvua"

njia

"barabara'' au "sehemu za kupita"

milipuko ya radi

"sauti ya radi." Hii ni sauti kuu ya radi ambayo hutoka katika mawimbi ya hewa.

kuifanya mvua inyeshe

Yahweh hutengeneza mifereji ya chemichemi ya maji ili kwamba aweze kutuma maji juu ya nchi sehemu ambazo hakuna watu.

hakuna mtu aishiye ndani yake

"sehemu isiyo na watu"

ili kutimiza mahitaji

"ili kwamba mvua iweze kukidhi mahitaji"

mikoa iliyo kame na yenye ukiwa

"sehemu ambazo hazina mimea au wanyama au watu"

majani mororo

majani ambayo kwanza yameanza kukua na bado machanga na laini

kuyastawisha

"kuanza kukua"

Job 38:28

Maelezo ya jumla

Yahweh anaendelea kumtia changamoto Ayubu.

Je kuna baba wa mvua? Ni nani aliyeyafanya matone ya umande?

Yahweh anatumia maswa haya kukazia kwamba Ayubu hafahau jinsi Yahweh anavyoitengeneza mvua, umande, barafu, na theluji

Je kuna baba wa mvua?

Yahweh anaiongelea mvua kana kwamba alikuwa ni mtu.

aliyeyafanya

kazi ya baba katika kumfanya mtoto azaliwe

matone ya umande

matone ya umande ambayo huunda mtonesho katika mmea na katika vitu vingine

Na ni nani aliyeizaa theluji nyeupe

"ambaye ameizaa theluji nyeupe"

Maji hujificha menyewe

katika kipindi cha masika barafu huficha maji chini yake.

vilindi

Hii hurejelea maji ya kina kirefu kama vile maziwa, mito, na bahari

Job 38:31

Maelezo ya jumla

Yahweh anaendelea kumtia changamoto Ayubu

Je unaweza kuzifunga minyororo.....juu ya dunia

Yahweh anatumia maswali haya kukazia kwamba Ayubu hajui jinsi ya kutawala na kuongoza nyota.

kuzifunga minyororo

"kukaza minyororo" au "kufunga vifungo"

Kilimia...Orioni...dubu

Haya ni majina ya makundi ya nyota.

kuvifungua vifundo vya Orioni

"kuvunja vifungo vinavyoshikilia Orioni"

nyota

Hii inarejelea aina kumi na mbili tofauti tofauti za nyota ambazo huonekana baada ya jua wakati linapozama. Mkusanyiko wa nyota huonekana nyuma ya jua kila mwezi.

kutokea katika nyakati zake

"ili kwamba zionekanae kwa wakati sahihi"

watoto wake

"vitoto vichanga vya dubu"

Job 38:34

Maelezo ya jumla

Yahweh anaendelea kumtia changamoto Ayubu

Je waweza kupaza....sisi tupo hapa

Yahweh anatumia maswali haya kukazi kwamba Ayubu hawezi kutawala mawingu, mvua au mwanga wa radi.

ili kwamba maji mengi ya mvua yakufunike

"ili kwlamba maji mengi sana yatakufunika"

Je waweza kuagiza miali ya mwanga ili itokee

"waweza kuamuru miali ya radi kutokea mahali unapotaka itokee na kwa kweli itatokea'

kukwambia

"na watakwambia"

Sisi tupo hapa

Kirai hiki kina maana, "sisi tupo hapa ili kwamba wewe utuambia kila unachotaka sisi tufanye"

Job 38:36

Maelezo ya jumla

Yahweh anaendelea kumtia changamoto Ayubu

Ni nani ameweka hekima...kushikama kwa pamoja

Yahweh anatumia maswali haya kukazi kwamba Mungu ana utawala juu ya mawingu na kwamba Ayubu hana uwezo huo

ameweka hekima katika mawingu

'ameyapa mawingu hekima" Yahweh anaelezea mawingu kana kwamba walikuwa ni watu na alikuwa ameyapa hekima ili kwamba yajue kile cha kufanya.

Nani anaweza kuyahesabu mawingu

Kirai hiki kina maana: "Ni nani awezaye kujua kuwa ni wembamba wa mawingu ni wa namna ganii katika anga"

viriba

Hivi ni vitu vilivyotengenezwa na watu ili viweze kuhifadhi maji. Yahweh anayarejeleamawingu mazito kama "viriba" kwasababu kwa kuwa yanashikilia maji mengi kama viriba vya maji.

wakati mavumbi yanapoungana kuwa kitu kigumu

"wakati matope ya mvua yanapoungana kwa pamoja kuwa kipande kimoja." Mvua huyafanay mavumbi makavu yaungane kwa pamoja kama kipande kimoja cha udongo.

mabonge ya dunia yanaposhikama kwa pamoja

Vipande vya udongo hushikana kwa pamoja"

Job 38:39

Maelezo ya jumla

Yahweh anaendelea kumtia changamoto Ayubu

Je waweza kuwinda... kulala katika hali ya kuvizia

Yahweh anatumia maswali haya kukazia kwamba yeye anajua jinsi ya kulisha simba, lakini Ayubu hajui.

mawindo

"nyara" Huyu ni mnyama ambaye anaweza kuliwa na simba

simba jike

Huenda ni "simba"

au kutosheleza hamu ya watoto wadogo wa simba

"au kuwapa simba wadogo chakula cha kutosha ili kwamba waweze kuishi"

watoto wake wadogo

"simba wadogo." Hawa ni simba wadogo ambao wana umri unaotosha kuwinda wao wenyewe.

katika pango lao

"katika sehemu ambazo wanaishi" au "sehemu za makao yao"

kukaa katika kificho

"kulala katika uoto wa mimea minene"

kulala katika hali ya kuvizia

"ambayo ni sehemu ya kuvizia" au "ni sehemu ambayo wanajificha ili kukamata wanyama wengine." Simba hujificha katika katika mimea minene na kusubiria mnyama apite na ili wamrukie na kumkamata mnyama huyo.

Job 38:41

Maelezo ya jumla

Yahweh anaendelea kumtia changamoto Ayubu

aletaye mawindo

Yahwe anatumia swali hili kukazi kwamba ni yeye aletaye chakula kwa kunguru na ya kwamba Ayubu halijui hilo.

mawindo

mnyama ambaye kunguru humtafuta na anaweza kumla

kunguru

ndege aina ya kunguru

wanapomlilia Mungu

"kumlilia Mungu ili kupata msaada" au " kumlilia Mungu ili awaokoe"

kutangatanga

"kuzunguka zunguka"

kwa kukosa chakula

"kwasababu hawana chakula" au "kwa kuwa hawana kitu cha kula"

Job 39

Job 39:1

Maelezo ya jumla

Yahweh anaendelea kumtia changamoto Ayubu.

Je unajua ni wakati gani .... muda ambao huzaa watoto wao

Yahweh anatumia maswali haya kutia mkazo kwamba anatunza mbuzi na paa ilihali Ayubu hawezi kufanya hivyo.

Je waweza kuwangalia paa wakati wanapozaa watoto wao?

"wakai paa wanapozaa je waweza kuhakikisha kwamba kila kitu kinaenda sawa"

wanapozaa watoto wao

"kuzaa"

"kuhesabu miezi ya kuchukua mimba

"kuhakikisha kuwa wanakamilisha muda wa mimba zao"

wa....

Kiambishi hiki kinarejelea mbuzi na paa

muda ambao huzaa watoto wao

wakati wao wa kuzaa"

Job 39:3

Maelezo ya jumla

Yahweh anaendelea kumtia changamoto Ayubu

Wanainama chini

Kiambishi 'wa'inarejelea mbuzi na paa

kuzaa watoto wao

"kuwafanya watoto wao watoke ndani yao"

kisha maumivu yao ya uzazi yanaisha

Maneno "maumivu ya uzazi' yanarejelea uzao wa mbuzi na paa kwasababu ni matokeo ya kazi na maumivu ya mama zao.

uwanda wa wazi

"nchi ya mashamba" au "porini"

hawarudi tena

"hawatarudi tena kwao" au " kurudi kwa mama zao"

Job 39:5

Maelezo ya jumla

Yahweh anaendelea kumtia changamoto Ayubu

nani.....nchi ya chumvi

Yahweh anatumia maswali haya ili kutia mkazo kwamba yeye huwalinda punda pori na ya kwamba Ayubu hawezi kufanya hivyo.

Punda mwtu.... punda wepesi

Haya ni majina tofauti ya aina ile ile ya punda

vifungo

kamba, minyororo ambayo hufunga mnyama na kumzuia asikimbie.

ni nyumba ya nani

Yahweh anaiongolea punda kana kwamba alikuwa ni mtu ambaye ana nyumba. "Nilimpta Araba kama nyumba ya kuishi"

nchi ya chumvi

nchi inayoizunguka Bahari ya Chumvi ambayo ina chumvi nyingi ndani yake.

Job 39:7

Maelezo ya jumla

Yahweh anaendelea kumtia changamoto Ayubu

hu...

Kiambishi hiki kinarejelea punda mwitu

Hucheka kwa dharau

Yahweh anaiongelea punda kana kwamba alikuwa ni mtu. Punda walichekka kwasababu wale walikuwa katika mji lazima wasikie sauti kubwa, ingawa alikuwa akiishi sehemu ya ukimya.

mwongozaji

mtu ambaye anawalazimisha wanyama kufanya kazi.

malisho

sehemu ambazo wanyama wanaweza kula mimea inayokua katika mashamba

Job 39:9

Maelezo ya jumla

Yahweh anaendelea kumtia changamoto Ayubu

je nyati...bonde kwa ajili yako?

Yahweh anatumia maswali haya ili kutia mkazo kwamba Ayubu hawezi kuwatawala nyati.

Nyati

Maana zinazowezekana ni 1) "ng'ombe wa porini" 2)"swala" aina fulani ya swala anayeonekana kama ng'ombe dume.

kuwa na furaha

"kuridhia"

atakubali kukaa katika zizi lako

"kukaa karibu na zizi wakati wote wa usiku"

hori/zizi

Katika mazingira ya Israeli, hiki kilikuwa ni chombo cha kulishia wanyama

mtaro

Ni mfereji mrefu uliotengenezwa katika sehemu chafu kwa kutumia plau.

kuchimba

"kulima kwa plau"

kwa ajili yako

"nyuma yako" wakati wa kulima kwa plau, mtu huongoza ng'ombe akiwa nyuma yake.

Job 39:11

Maelezo ya jumla

Yahweh anaendelea kumtia changamoto Ayubu

waweza kumtumaini...uwanda wako wa kupuria

Yahweh anatumia maswali haya ili kutia mkazo kwamba Ayubu hawezi kuwatawala nyati.

kumtumaini

Kiambishi 'm' kinamrejelea 'nyati"

kumwachia kazi yako ili aifanye

"umwachie yeye aifanye kazi yako ngumu kwa ajili yako"

Job 39:13

Maelezo ya jumla

Yahweh anaendelea kumtia changamoto Ayubu

Mabawa... ya upendo

Yahweh anatumia swali hii ili kutia mkazo kwamba Ayubu hawezi kuelezea kwanini mbuni wanaenenda jinsi wanavyofanya.

mbuni

huyu ni ndege mkubwa ambaye anaweza kukimbia haraka, lakini hawezi kupaa.

kwa majivuno

"kwenda kwa furaha"

mabawa

haya ni manyoya marefu juu ya mabawa ya ndege

manyoya

ni manyoya madogo yaliyoenea juu y mwili wote wa ndege

yana upendo

Maana zinazowezana 1) "uaminifu" 2) "ya kurungu" Jina hili lilimaanisha "mwaminifu mmoja" au mwenye kupenda, kwasababu kunguru huwajali sana watoto wake.

katika nchi

juu ya ardhi

kuyaharibu

Neno hili linarejelea mayai.

kuyakanyaga

"kukanyaga juu yao"

Job 39:16

Huyatendea vibaya

kiambishi 'hu' kinamrejelea mbuni jike

kazi yake

kazi ile ambayo huifanya wakati wa kulalia mayai na kuwahudumia vifaranga.

yaweza kupotea bure,

kama watoto watakufa, kazi yake yote itakuwa ni bure

amemnyima hekima

humfanya asahau hekima

ufahamu

Angalia ulivyofasiri katika 11:4

huwacheka...mpanda farasi wake

Ina maana kwamba hucheka kwasababu huenda kwa kasi kulliko farasi. "Hucheka... kwa mpanda farasi wake, kwasababu farasi hawezi kukimbia kwa kama yeye.

Job 39:19

Maelezo ya jumla

Yahweh anaendelea kumtia changamoto Ayubu

Je umempa farasi ... panzi?

Yahweh anatumia maswali haya kutia mkazo kwamba ni yeye ndiye huyafanya mambo haya ambayo Ayubu hayawezi.

umeivika shingo yake

Neno 'kuvika" ni njia ya kuelezea jinsi ambavyo Yahweh alivyoifanya shingo ya farasi.

manyoya yake

ni nywele ndefu ambazo hushuka chini kutoka katika shingo ya farasi na hutisika wakati farasi anapoondoka.

nzige

ni aina kubwa ya panzi ambayo yaweza kuruka kwenda mbali na kwa haraka sana.

mlio

ni sauti kubwa ambayo farasi huitoa katika pua zao.

Job 39:21

Hurarua

Kiambishi 'hu' kinarejelea farasi. Farasi huchimbua ardhi kwasababu anakuwa amesisimka kuanza kupigana.

hurarua

"kuchimbua ardhi kwa kutumia kwato"

hudharau

"kuchekelea"

hashangazwi

"kuogopeshwa'' au ''kuhofu''

harudi nyuma

"hakimbii mbali''

podo

ni chombo ambacho hutunza mishale

hugongagonga

"kutikisika na kutoa kelele''

ubavuni

sehemu za pembeni za farasi

fumo

ni mti mrefu uliochongoka mwishoni ambao watu huurusha kwa maadui zao.

Job 39:24

huimeza

Kiambishi 'hu' kinarejelea farasi

huimeza nchi

Farasi hukimbia kwa kasi juu ya ardhi na ya kwamba nchi hupita kama mtu anakunywa maji.

hasira na ghadhabu

"kwa miondoko mikubwa na ya haraka" Farasi anaposisimuka huondoka kwa haraka na kwa nguvu. Na kwasababu hii, farasi hukimbia kwa haraka.

katika sauti ya tarumbeta,

"wakati mtu fulani anapopuliza tarumbeta ili kutangaza kwamba vita imeanza."

hawezi kusimama sehemu moja

"mara kwa mara huwahi kwenye vita"

husema Ooo!

Watu hutoa Sauti Ooo! wakati wanapokuwa wamefurahia kitu fulani. Farasi huwa na furaha kwasababu huifurahia vita.

vishindo vya radi

Hii ina maana kwamba farasi huvisikia vitu hivi. "husikia sauti ya radi"

kelele

"Vita hupiga kelele" Watu huwa na kilio maalumu ambacho hukitumia kuonesha kuwa wao ni watu gani na nguvu zao kuu na ujasiri na kuwaogopesha maadui.

Job 39:26

Je ni kwa hekima ... kwa upande wa kusini?

Jibu lililofika la swali hili ni "hapana". Si kwa hekima yetu..."

Je ni kwa hekima yako kwamba mwewe hupaa

"si wewe unayemfunza mwewe kuruka"

huyanyosha mabawa yake

hupaa

kwa upande wa kusini

Katika jiografia ya kibiblia, ndegu hupaa na kuelekea upande wa kusini katika kipindi cha masika ili kuishi katika hali ya joto.

Job 39:27

Je ni kwa agizo lako ... kiota chake katika sehemu za juu?

Jibu lililofichika la swali hili ni ''hapana'' ''si kwa maagizo yako....kiota katika sehemu za juu"

Je ni kwa agizo lako

"je ni kwasababu wewe unaiambia kufanya hivyo"

huruka juu

"hupaa juu angani"

majabali

ni vifusi virefu ni makao ya tai kwasababu wanyama ambao wangetaka kuwala hawawezi kuwafikia.

Job 39:29

hutafuta mawindo

Kiambishi 'hu' kinarejelea tai

macho yake huyaona

huwaona wao

pale walipo wafu

"sehemu palipo na watu wafu'' Kirai hichi kinarejelea maiti zilizolala katika sehemu wazi, si miili iliyozikwa ardhini.

ndipo na yeye alipo.

"yuko pale kuwala wao"

Job 40

Job 40:1

Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi?

Jibu linalotarajiwa hapa ni, 'hapana'

Job 40:3

mimi si mtu muhimu;

sina umuhimu

je nawezaje kukujibu?

"Siwezi kukujibu"

Job 40:6

Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume

Hii humlinganisha Ayubu na mtu anayejiweka tayari kwa ajili ya kazi. ''Jifunge mkanda kiunoni mwako'' ina maana ya kujifunga kipande cha nguo katika sehemu ya mkanda ili mtu aweze kufaya kazi.

Job 40:8

Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki?

Unasema mimi si mwenye haki"

je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?

Unanihukumu mimi ili wewe uweze kusema kwamba wewe ni mwenye haki."

mkono kama wa Mungu

"nguvu kama nguvu za Mungu

Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?

"Hakika hauna sauti ya nguvu kama ya Mungu, ambaye huileta radi.

Job 40:10

Sambaza ziada ya hasira yako

"Funua jinsi hasira yako ilivyo katika majivuno ya watu"

mtazame kila mmoja mwenye kiburi

"angalia watu wote wenye kiburi"

umshushe chini.

"mweke chini katika umuhimu"

Job 40:12

zifunge nyuso zao

"wafunge hao"

katika sehemu zilizositirika

Hii ni njia nyingine ya kusema 'sheoli' au sehemu ambapo watu wa agano la kale walienda baada ya kufa.

Job 40:15

anakula

Kiambishi 'a' kinarejelea kiboko.

kama ng'ombe

Hii inaelezea jinsi ambayo kiboko anavyokula majani

Job 40:17

kama mti wa mwerezi

"namna ambayo matawi ya mierezi yanavyokwenda.'

kama ya mirija ya shaba

Mahali hapa, mifupa yake inalinganishwa na mirija iliyotengenezwa kwa shaba ili kuonesha jinsi mnyama alivyo mgumu

kama kipande cha chuma

Huu mlinganisho wa mwisho unaelezea nguvu za mnyama mkubwa.

Job 40:19

milima humpatia chakula

Mwandishi anaongelea juu ya milima kana kwamba walikuwa ni watu wanaoweza kumpatia chakula.

mimea ya kivuli

Mmea wa kivuli ni mmea wenye maua ambayo huelea juu ya maji katika sehemu zenye maji maji na tope

mianzi

Majani marefu ambayo hupatikana katika sehemu za maji maji na matope au mabwawa.

Job 40:22

miti yenye vivuli

angalia jinsi ulivyotafsiri hii katika 40:19

kingo

pande za mto

hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake

"hata kama gharika litakuja juu ya pua yake"

Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano... kwa mtego?

Hili ni swali hili la kejeli hupaswa kujibiwa kwa jibu la kukanusha. "Hakuna yeyote awezaye kumkamata kwa ndoano au kwa mtego"

Job 41

Job 41:1

Maelezo ya jumla

Mungu anaendelea kuzungumza. Anatumia maswali mengi ya kejeli kumtia changamoto Ayubu.

Au kumfunga taya zake kwa kamba?

"Hauwezi kumvua mamba kwa ndoano ya samaki"

Au kumfunga taya zake kwa kamba?

Hii si sentensi kamili, lakini maana yake yaweza kufahamika kutoka katika muktadha kama " Au kumfunga taya zake kwa kamba? "au hauwezi kumfunga taya kwa kamba.

Je waweza kuweka kamba katika pua zake

"Hauwezi kuweka kamba katika pua yake, au kuchoma taya zake kwa ndoano"

Je atafanya maombi mengi kwako?

"Hawezi kufanya maombi kwako"

Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?

"Hataweza kuzungumza maneno laini"

Job 41:4

Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?

"Hatafanya agano na wewe, kwamba hautamfanya kuwa mtumishi milele"

Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege?

"Hautacheza naye kama ambavyo ungecheza na ndege"

Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?

"Hautamfunga kwa ajili wa watumishi wako wa kike"

Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara?

"Makundi ya wavuvi hawataweza kufanya biashara naye"

Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?

"Hawatamgawanya kwa wafanya biashara"

watamgawanya

"maundi ya wavuvi watamgawanya"

Job 41:7

e waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?

"Hauwezi kumchoma ngozi yake kwa silaha za kuwindia, wala kumchoma kichwa chake kwa zana za kuvulia"

vyusa au kichwa cha mikuki

chusa ni mkuki mkubwa ukiwa umechongoka ukitumika kuwindia samaki wakubwa au nyangumi.

je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?

"kila mmoja atatupwa chini ardhini mbele yake"

Job 41:10

Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?

"Hakuna yeyote anayeweza kusimama mbele yangu/yake"

Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa?

"Hakuna yeyote ambaye kwanza amenipa kitu fulani, ili kwamba niweze kumlipa.

Sitanyamaza kimya

"Hakika nitasema"

miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake

"mguu. Nitazungumza pia juu ya mambo yanayohusu nguvu zake"

nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.

"nguvu. Nitazungumzia pia juu ya umbo lake la neema"

Job 41:13

Nani awezaye kuiondoa ngozi yake?

"hakuna yeyote anayeweza kuondoa nguo yake ya nje"

Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?

"Hakuna awezaye kumchoma katika ngovi yake nene"

Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?

Hakuna yeyote anaweza kuyapanua makanwa yake...yanaogofya"

yamefungwa kwa pamoja kama chapa

Hii ina maana kwamba magamba yamekaribiana kwa ukaribu na yameungana kwa pamoja.

Job 41:16

Moja li karibu na jingine

safu moja ya kinga iko karibu na nyingine.

hayawezi kutenganishwa

"watu hawawezi kuwatenganisha"

Job 41:19

Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje

"katika mdomo wake hutoka miali, cheche za moto zikiruka nje ya mdomo wake." Mungu anafafanua wazo lile lile kwa njia mbili tofauti ili kutia mkazo juu ya mwonekano wa kutisha wa mamba.

Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana

Kutoka kwa moshi katika pua zake kunalinganishwa na chungu kinachochemshwa juu ya moto.

Job 41:22

yake...hu

Maneno ''yake'' na ''hu'' yanamrejelea mamba

haziwezi kuondolewa

"hakuna yeyote awezaye kuyaondoa"

Job 41:25

hata miungu huogopa;

"Hata watu wenye nguvu huwa waoga"

Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu

"Hufikiri juu ya silaha zilizotengenezwa kwa chuma kana kwamba zilikuwa ni silaha zilizotengenezwa kwa majani makavu" Hii inaonesha jinsi ambavyo vyuma imara huwa dhaifa kwa mamba.

hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza

"'Hufikiri juu ya silaha zilizotengenezwa kwa fedha kana kwamba zilikuwa ni silaha zilizotengenezwa kwa mbao zilizooza."

Job 41:28

kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.

Hii ina kwamba mawe ya kombeo hayan matumizi tena kuliko makapi katika upepo dhidi ya mamba.

kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.

Hii ina maana kwamba rungu haitakuwa na faida tena kuliko makapi katika kumpiga mamba.

yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma

Mamba anafananishwa na mtu anayechekelea kushindana naye kusiko na maana kwa kumrushia mikuki.

Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu

Hii inazungumzia juu ya magamba yaliyo na ukali.

huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.

Sentensi hii inalinganisha mkia wake na chombo cha kusagia ambacho husugua ardhi na kuacha alama kana kwamba kilikuwa kinaenda.

Job 41:31

Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto

"wakati anapopita katika ya maji, huacha mchirizo wa alama ukiotoa povu nyuma yake, kama ni chungu cha maji kilichochemka na kutoa povu."

huifanya bahari kama chungu cha lihamu

Hii ina maana kwamba husuka suka bahari kama chupa ya marihamu ambavyo ingeonekana baada ya kutikiswa hasa.

mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.

Hii ina maana kwamba maji yote hupinduliwa juu wakati mamba anapoogelea kwasababu ya ukubwa wake, naye husababisha mchirizo wa alama ukitoa mapovu.

Job 41:33

Hakuna cha kumlinganisha

"hakuna kiumbe kingine kama mamba"

Hukiona kila kitu chenye kiburi

"yeye ana kiburi sana sana"

yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.

"Mamba ni kama mfalme wa viumbe vyenye kiburi"

Job 42

Job 42:1

"Ninajua kwamba unaweza kufanya mambo yote, ya kuwa hakuna kusudi lako linaweza kuzuiliwa.

"Ninajua kwamba wewe unaweza kufanya mambo yote. Ninajua kwamba hakuna kusudi lako lolote linaweza kuzuiliwa." Hili ni wazo lile lile limeelezwa kwa jinsi mbili tofauti.

hakuna kusudi lako linaweza kuzuiliwa

"hakuna yeyote awezaye kuzuia kusudi lako lolote"

Ni nani huyo ambaye pasipo maarifa huificha mipango?

Matoleo mengi ya kisasa hukubaliano kwamba Ayubu ananukuru maneno ya Mungu kutoka katika 38:1. Wafasiri wanaweza kuamua kuiweka wazi kwamba Mungu alimwuliza swali hili Ayubu, na ya kwamba Ayubu kwa sasa analikumbuka.

huificha mipango

Hii ina maana kwamba, kuficha au kutoiwakilisha mipango ya Mungu na ushauri wake.

Job 42:4

lakini sasa jicho langu linakuona wewe

"lakini sasa ninakufahamu wewe"

ninatubu kwa mavumbi na majivu

Hii ni njia ya kiutamaduni ya kuonesha majuto na toba

Job 42:7

Ilitokea baada ya kuwa

Kirai hiki kimetumika hapa kuonesha tukio kubwa katika habari hii. Kama lugha yako ina jinsi ya kuweza kusema hili unaweza kutumia.

Elifazi Mtemani

angalia ulivyofasiri hii katika 2:1

mafahari saba

mahafari 7

Bildadi Mshuhi

Angalia jinsi ulivyofasiri hii katika 2:11

Zofari Mnaamathi

Angalia jinsi ulivyofasiri hii katika 2:11

Mungu alimtakabali Ayubu

"Mungu anaipokea sala ya Ayubu kwa ajili ya marafiki zake watatu"

Job 42:10

Waliomboleza pamoja naye na walimfariji

Hizi kazi mbili za kuomboleza na kufariji hufanya kazi pamoja katika mchakato wa kumrejesha Ayubu.

Job 42:12

kuliko mwanzo wake

"zaidi sana kuliko sehemu ya kwanza ya maisha yake"

kondoo kumi na nne elfu

kondoo 14,000/=

ngamia elfu sita

ngamia 6,000

jozi elfu moja

jozi za ng'ombe 1,000

wana saba na mabinti watatu.

wana 7 na binti 3

Yemima

binti wa kwanza wa Ayubu

Kezia

binti wa pili wa Ayubu

Kerenihapuki

binti wa tatu anaitwa Kerenihapuki

Job 42:15

hawakupatikana wanawake wazuri kama mabinti wa Ayubu.

"Mabinti za Ayubu walikuwa wazuri zaida kuliko wanawake wengine" au "mabinti za Ayubu walikuwa ni wazuri sana"

akiwa mzee na akijawa na siku nyingi.

Maneno "kujawa na siku" kimsingi yanamaanisha kitu kile kile ya kuwa 'mzee" Virai hivi viwili vinatengeneza nahau moja "kuwa mtu mzee sana"

Psalms 1

Psalms 1:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

ambaye hatembei katika ushauri wa waovu

"Ushauri wa waovu" unazungumziwa kana kwamba ni njia ya kufuata. "ambaye hafuati ushauri wa waovu"

kusimama katika njia ya watenda dhambi

Hapa neno "njia" inaonesha namna watu wanavyoishi. Neno "simama" liko sambamba na "tembea." "kuiga tabia za watu watenda dhambi"

au kuketi katika kusanyiko la wenye dhihaka

Kuketi na watu wanao mdhihaki Mungu inaonesha kuwaunga watu wanao mdhihaki Mungu. "au kuwaunga wale wanao mdhihaki Mungu" au "au kumdhihaki Mungu na wale wanaomdhihaki"

furahi

"kuridhika" au "furaha"

Yahwe

Hili ni jina la Mungu ambalo alilifunua kwa watu wake katika Agano la kale.

Psalms 1:3

Taarifa ya Jumla:

Kifungu hiki kinatambulisha picha iliyo fafanuliwa kwa undani ambayo mtu mtakatifu anawaziwa kama mti unao stawi.

Atakuwa kama mti ... matunda katika msimu wake

Katika Biblia, watu mara nyingi wanazungumziwa kama miti. Watu wanaofurahi katika sheria ya Yahwe wanaweza kufanya yote ambayo Mungu anataka wafanye kama mti uliopandwa kandokando ya maji uwezavyo kutoa matunda mazuri. "Atafanikiwa kama mti ... matunda katika msimu wake"

uliopandwa kandokando ya vijito vya maji

Mti ulipandwa kandokando ya kijito unaweza kupata maji ya kutosha kuwa na afya.

unaotoa matunda yake katika msimu wake

Miti yenye afya inatoa matunda mazuri kwa wakati sahihi.

ambao majani yake hayakauki

Mti ukipaata maji yakutosha, majani yake hayakauki na kufa.

chochote afanyacho kinafanikiwa

"atafanikiwa kwa chochote afanyacho"

Psalms 1:4

Waovu hawako hivyo

Jinsi wasivyo hivyo inaweza kuwekwa wazi. "Waovu hawana mafanikio" au "Waovu hawafanikiwi"

lakini ni kama makapi

Jinsi walivyo kama nyasi inaweza kuwekwa wazi. "lakini hawana faida kama makapi"

hawatasimama katika hukumu

Kupona wakati Mungu anahukumu inazungumziwa kama "kusimama." "hawatapona wakati Mungu anawahukumu" au "watalaaniwa Mungu atakapo wahukumu"

wala watenda dhambi katika kusanyiko

"wala watenda dhambi kusimama katika kusanyiko"

wala watenda dhambi katika kusanyiko la wenye haki

Kukubaliwa na Mungu kama mwenye haki inazungumziwa kama kusimama na kundi la watu wenye haki. "na Mungu hatawakubali watenda dhambi pamoja na watu wenye haki"

Psalms 1:6

Kwa kuwa Yahwe anakubali njia ya watakatifu, bali njia ya waovu itapotea

Vishazi hivi viwili vinaonesha tofauti kwa yale yanayowatokea watu watakatifu na yale yanayowatokea watu waovu.

njia ya mwenye haki

Jinsi watu wanavyoishi inazungumziwa kama vile ni "njia" au "barabara" ambayo walikuwa wakitembea. "jinsi wenye haki wanavyoishi"

njia ya waovu itapotea

Hapa "njia" inamaanisha waovu, ambao kimafumbo wanatembea katika hiyo njia. "Waovu wataangamia kwa sababu ya njia yao" au "waovu watakufa kwa sababu ya jinsi wanavyoishi"

Psalms 2

Psalms 2:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa nini mataifa yako katika ghasia ... kwa nini watu wanafanya mipango itakayoshindwa?

Vishazi hivi viwili vina maana zakufanana, na "mataifa" na "watu" linamaanisha kundi hilo hilo la watu. Maneno "mataifa" na "watu" yanaweza kumaanisha viongozi wao. "Kwa nini viongozi wa mataifa wako katika ghasia na kufanya mipango itakayoshindwa?"

Kwa nini mataifa yako katika ghasia, na kwa nini watu wanafanya mipango itakayoshindwa?

Maswali haya yanatumika kuonesha mshangao kwamba watu wanafanya jambo baya sana na laki pumbavu. "Mataifa yako katika ghasia na watu wanafanya mipango itakayoshindwa."

mataifa yako katika ghasia

Hii inaweza kumaanisha kuwa mataifa yalikuwa yakifanya vurugu ya kelele na hasira.

mipango itakayoshindwa

Hii inawezekana kuwa mipango dhidi ya Mungu na watu wake.

Wafalme wa nchi wafanya msimamo wa pamoja ... viongozi wao wanafanya njama pamoja.

Vishazi hivi viwili vina maana ya kufanana.

wafanya msimamo wa pamoja

"kukusanyika kupambana" au "kuungana na kujiaanda kupinga"

Tupasue pingu ... tutupe minyororo yao

Watu wa mataifa mengine wanamzungumzia utawala wa Yahwe na Masihi juu yao kama pingu na minyororo. "Tujiweke huru kutoka kwenye utawala wao; tusiwaruhusu watutawale tena!"

Psalms 2:4

Yeye ... Bwana

Maneno haya yanamaanisha Yahwe. Yahwe mara nyingi huitwa "Bwana" lakini maneno kwa ajili ya "Yahwe" na "Bwana" ni tofauti.

aketiye mbinguni

Hapa kuketi inamaanisha kutawala. Kile anachokalia kinaweza kuelezwa vizuri. "anatawala mbinguni" au "anaketi katika kiti chake cha enzi mbinguni"

Bwana anawadhihaki

"Bwana anawadhihaki hao watu." Kwa nini anawadhihaki inaweza kuelezwa vizuri. "Bwana anawadhihaki kwa mipango yao yakipumbavu"

na kuwatisha katika gadhabu yake

"gadhabu" inamaanisha kuwa na hasira kali.

kuwatisha

"kuwaogofya"

Psalms 2:6

Mimi mwenyewe

Yahwe anasisitiza kuwa yeye, na sio mtu mwingine, ndiye aliyemtia mafuta mfalme wake.

mtia mafuta mfalme wangu

"kumchagua mfalme wangu kutawala"

Nitatangaza amri ya Yahwe

Mtu anayesema haya ni mfalme. Hii inaweza kuelezwa vizuri. "Mfalme anasema, 'Nitatangaza amri ya Yahwe'"

Akaniambia

"Yahwe akaniambia"

Wewe ni mwanangu! Siku hii nimekuwa baba yako

Kati ya watu wengi katika sehemu hiyo ya dunia kipindi hicho, wanaume waliweza kuamua kupanga watoto kisheria, ambao watakuwa warithi wao. Hapa Yahwe anamtwaa mwanamme na kumfanya kuwa mfalme wa Israeli. "Nitakufanya mwanangu. Siku hii nimekuwa baba yako" au "Sasa u mwanangu na mimi baba yako"

Psalms 2:8

Kauli Unganishi:

Yahwe anaendelea kuzungumza na mfalme mpya wa Israeli.

mataaifa kwa urithi wako ... sehemu za mbali za nchi kwa mali yako

Mafungu haya yanaonesha mawazo ya kufanana sana.

sehemu za mbali za nchi

"ardhi iliyo mbali kabisa"

Utawavunja kwa fimbo ya chuma; kama chupa ya mfinyanzi, utawaponda vipande vipande.

Vifungu hivi vinanaonesha mawazo ya kufanana sana.

Utawavunja kwa fimbo ya chuma

Kuyashinda mataifa inazungumziwa kama kuyavunja, na nguvu yake inazungumziwa kama fimbo ya chuma. "Utawashinda kabisa kwa nguvu yako"

utawaponda vipande vipande

Kuangamiza mataifa inazungumziwa kana kwamba yanaweza kupondwa kama chupa ya udongo. "utawaangamiza kabisa kama chuma ya udongo"

chupa ya mfinyanzi

Mfinyanzi ni mtu anayetengeneza vyungu vya udongo na chupa. Hizi ni nyepesi kuvunjika. "chupa ya udongo" au "chungu cha udongo"

Psalms 2:10

Kwa hiyo sasa, nyie wafalme, muonywe; muwekwe sasa, nyie watawala wa nchi

Mafungu haya mawili yana maana za kufanana. "Kwa hiyo sasa, nyie wafalme na watawala wa nchi, muonywe na kurekebishwa"

muonywe

Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "sikiliza onya hili" au "muwe na hekima"

muwekwe sasa

Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "sikiliza masahihisho haya" au "chukua masahihisho haya"

Psalms 2:12

Mbusu mwana

Watu walimwonesha mfalme wao kuwa walikuwa waaminifu kwake kwa kumbusu, labada miguuni. "Mwonesheni mwana kuwa kweli ni waaminifu kwake" au "Sujuduni kwa unyenyekevu kwa mwanaye"

mtakufa njiani

Hii inaweza kumaanisha kufa hapo hapo, kabla hajapata nafasi ya kuondoka. "utakufa hapo hapo"

hasira yake inapowaka kwa muda tu

Hasira ya mfalme inazungumziwa kama vile ni moto unaoweza kuwaka. "anapokasirika sana ghafla"

wanaotafuta usalama kwake

Kumuomba mfalme ulinzi inazungumziwa kama kutafuta usalama kwake. "wanaomuomba mfalme kuwalinda"

Psalms 3

Psalms 3:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Yahwe, maadui zangu ni wangapi!

Tamko hili linaonesha kuwa Daudi anawaogopa maadui wake. "O Yahwe, nina maadu wengi sana!"

wameinuka dhidi yangu

Kupigana na mtu inazungumziwa kama kuinuka dhidi yake. "wamekuja dhidi yangu"

Sela

Hili linaweza kuwa neno la kimuziki linalowaongoza watu jinsi ya kuimba au kujecheza vyombo hapa. Tafsiri zingine huandika neno hili la Kiebrania, na zingine haziliweki.

Psalms 3:3

wewe, Yahwe, ni ngao yangu

Ngao humlinda askari. Daudi anazungumza kana kwamba Mungu ni ngao inayomlinda. "wewe, Yahwe, unanilinda kama ngao"

utukufu wangu

"wewe ni utukufu wangu." Kwa kumuita Mungu utukufu wake, Daudi anasema kuwa Mungu ndiye anayempa utukufu. Kwa kuwa Daudi amemaliza tu kuwazungumzia maadui zake na Mungu kuwa mlinzi wake, inawezekana alimaanisha kuwa Mungu anampa utukufu kwa kumpa ushindi juu ya maadui wake. "wewe ndiye unipaye utukufu" au "wewe ndiye unipaye ushindi"

unayenyanyua kichwa changu

"wewe ndiye unayenyanyua kichwa changu." Kumpa mtu ujasiri inazungumziwa kama kumnyanyua kichwa chake. "unayenitia moyo"

Nainua sauti yangu

Mtu kutumia sauti yake kulia inazungumziwa kama kuinua sauti yake.

Sela

Hili linaweza kuwa neno la kimuziki linalowaongoza watu jinsi ya kuimba au kujecheza vyombo hapa. Tafsiri zingine huandika neno hili la Kiebrania, na zingine haziliweki.

Psalms 3:5

waliojipanga dhidi yangu kila upande

"wamenizunguka kuniangamiza"

Psalms 3:7

Inuka

Daudi anazungumzia kuanza kufanya kitu kama kuinuka. "Chukua hatua" au "Fanya kitu"

utawapiga maadui wangu wote ... utavunja meno ya waovu

Vifungu hivi vinasema vitu vya kufanana sana. Misemo "maadui wangu" na "waovu" inamaanisha kundi moja la watu.

Kwa kuwa utawapiga maadui wangu kwenye taya

Hii ilikuwa ni njia ya kuwatukana watu. Daudi anazungumza kana kwamba Yahwe atakuja na kuwapiga kimwili adui zake. "Kwa kuwa utawafedhehesha adui zangu wote kama mtu anawapiga kwenye taya.

utavunja meno ya waovu

Wanyama huvamia kwa meno yao. Kuvunja meno yao inawaondolea nguvu ya kuvamia. Daudi anazungumza kana kwamba Yahwe atakuja na kupambana kimwili na waovu. "utawafanya waovu washindwe kunidhuru kama mtu kuvunja meno ya mnyama mkali"

Wokovu unatoka kwa Yahwe

Nomino dhahania ya "Wokovu" inaweza kuelezwa na kitenzi "okoa." "Yahwe anawaokoa watu wake"

Psalms 4

Psalms 4:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

kwenye vyombo vya nyuzi

"watu wanapaswa kucheza vyombo vya nyuzi na wimbo huu"

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Nijibu ninapoita

"Nisaidie ninapoita"

Mungu wa haki yangu

"Mungu, unayeonesha kuwa ni mwenye haki"

nipe nafasi ninapozungukwa

Kuwa hatarini inazungumziwa kama kuwa katika nafasi finyu. "niokoe ninapokuwa hatarini"

Psalms 4:2

Taarifa ya Jumla:

Daudi anaimba sehemu hii ya wimbo kana kwamba anazungumza na adui zake.

Nyie watu, mtageuza heshima yangu kuwa aibu hadi lini?

Daudi anatumia swali hili kuwakemea adui zake. "Nyie watu mnaendela kugeuza heshima yangu kuwa aibu!"

mtageuza heshima yangu kuwa aibu

Kumwaibisha badala ya kumheshimu inazungumziwa kama kuifanya heshima yake kuwa aibu. "kuniaibisha badala ya kuniheshimu" au "kuniletea aibu badala ya kuniletea heshima"

Hadi lini mtapenda kile kisicho na dhamani na kutafuta uongo?

Daudi anatumia swali hli kuwakemea adui zake. "Mnaendela kupenda vitu visivyo na dhamani na kutafuta uongo."

mtapenda kile kisicho na dhamani ... kutafuta uongo

Misemo hii miwili inamaana ya kufanana. Uongo hauna dhamani. "mtapenda uongo usio na dhamani"

Yahwe anawatenga watauwa kwa ajili yake

"Yahwe anawachagua watauwa kwa ajili yake"

Psalms 4:4

Mtetemeke kwa hofu

Uhusiano kati ya "kutetemeka" na "hofu" na ni nani watu wanapaswa kumhofu unaweza kuelezwa vizuri. "Mche Yahwe sana hadi utetemeke" au "Simama kwa kumshangaa Yahwe"

Mtetemeke

"Mtikisike"

Tafakari moyoni mwako

Moyo unaashiria mawazo ya mtu. Kuwaza kwa umakini inazungumziwa kama kutafakari ndani ya moyo wa mtu. "Waza kwa umakini:

Toa sadaka za haki

"Toa sadaka zilizo sawa"

weka imani yako kwa Yahwe

Imani inazungumziwa kama vile ni kitu kinachoweza kuweka sehemu. "muamini Yahwe"

Psalms 4:6

Nani atatuonesha chochote kizuri?

Swali hili linatumika kwa mojawapo kati ya kuuliza kwa ajili ya kitu au kuonesha matamanio kuhusu jambo ambalo bado halijatokea. "Tafadhali tuonesha jambo zuri" au "Tunatamani mtu atuoneshe jambo zuri"

Nani atatuonesha chochote kizuri?

Kuonesha kitu kizuri inaweza kumaanisha kuleta vitu vizuri au kusema kwamba vitu vizuri vimetokea. "Nani ataleta vitu vizuri kwetu?" au "Nani atasema kwamba kitu chochote kizuri kimetokea?"

inua mwanga wa uso wako kwetu

Mwandishi anamzungumzia Yahwe kuwatendea mazuri kana kwamba uso wa Yahwe ulimulika mwanga kwao. "kutenda mema kwetu"

Umeupa moyo wangu furaha zaidi

Moyo unaashiria mtu. "Umenipa furaha zaidi"

Umeupa moyo wangu furaha zaidi kuliko wengine walivyo

Furaha inazungumziwa kama kitu kinachoweza kupewa. "Umenifanya kuwa mwenye furaha zaidi kuliko wengine"

nafaka zao na divai yao mpya inapozidi

"Divai mpya" inaweza kumaanisha mizabibu. "wanapovuna mavuno mengi ya nafaka na mizabibu"

Ni kwa amani nitalala chini

Amani inazungumziwa kana kwamba ni sehemu. "Nitakuwa na amani ninapolala chini" au "Sitaogopa hatari ninapolala"

unanifanya salama

"unanifanya salama

Psalms 5

Psalms 5:1

Taarifa ya Jumla

Usambamba ni jambo la kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

na vyombo vya upepo

"Wimbo huu unapaswa kuandamana na watu wanaocheza vyombo vya upepo

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Sikia wito wangu kwako

Huu ni wito wa msaada. "Nisikie mimi ninapokuita sasa kwa ajili ya msaada"

sauti ya kulemewa

sauti ndogo watu wanazofanya wanapohangaika

asubuhi unasikia kulia kwangu ... asubuhi nitaleta dua yangu kwako

Vifungu hivi viwili vinamaana ya kufanana.

nitaleta dua yangu kwako

"Nitafanya ombi langu" au "Nitakuomba ninachohitaji"

kutazamia

"matumaini"

Psalms 5:4

Yahwe anawachuki watu wenye vurugu na waongo

Kwa kuwa Daudi anazungumza na Mungu katika zaburi hii, sentensi hii inaweza kuelezwa na neno "wewe." "Yahwe, wewe unawachukia watu wenye vurugu na waongo" au "Yahwe, wewe unachukia watu wanaofanya matendo ya vurugu na kuwadanganya wengine"

Psalms 5:7

nyumba yako

Hii inamaanisha hekalu la Mungu. "hekalu lako"

niongoze katika haki yako

Daudi anazungumzia haki kana kwamba ni njia na kufundisha kama kuongoza. Msemo "haki yako" unamaanisha kuwa Mungu ni mwenye haki. "nifundishe kufanya kilicho na haki kama wewe ufanyavyo"

nyosha njia yako mbele yangu

Daudi anazungumzia haki kana kwamba ni njia. Njia iliyonyoka ni rahisi kuona na kutemebelea. "nionesha vizuri jinsi ya kuisha njia sahihi" au "ifanye rahisi kwangu kufanya yaliyo sawa"

Psalms 5:9

Taarifa ya Jumla:

Daudi anawazungumzia adui zake

Kwa kuwa hakuna ukweli midomoni mwao

Ukweli kuwa midomoni mwao inamaanisha kuongea ukweli. "Kwa kuwa huwa hawasemi ya kweli"

utu wao wa ndani ni uovu

Utu wao wa ndani inamaanisha mawazo ya watu na tamaa zao. "mawazo yao na tamaa ni mbaya"

koo yao

Koo inaashiria maneno ya watu. "maneno yao" au "kile wanchosema"

koo yao ni kaburi lililo wazi

Koo yao inazungumziwa kana kwamba ni kaburi lililo wazi, tayari kwa ajili ya maiti kuwekwamo. Maana zinazowezekana ni 1) "wanasema watawaua watu" au 2) "Wanachosema huua watu"

wanijipendekeza na ulimi wao

"wanasema vitu vizuri kuhusu watu wengine bila kumaanisha"

ulimi wao

Ulimi unaashiria kile wanachosema watu.

njama zao ziwe anguko lao

"njama zao ziwasababishe kupitia maafa" au "wapunguze umuhimu wao kwa sababu ya njama zao"

njama

mipango ya kuwadhuru watu

anguko

Hili ni jambo linalowafanya watu kupitia maafa na kupoteza nguvu. Kupitia maafa au kupoteza umuhimu inazungumziwa kama kuangaku.

Psalms 5:11

wote wanaokukimbilia wafurahi

Mungu anazungumziwa kana kwamba ni kambi, sehemu ambayo watu wanaweza kulindwa. "Wote wanaokuja kwako kwa ulinzi wafurahi"

wote wanaokukimbilia wafurahi ... wapige kelele za shangwe kwa sababu unawalinda

Vishazi hivi viwili vina wazo la kufanana.

wanaokukimbilia

Kwenda kwa Yahwe kwa ajili ya ulinzi kunazungumziwa kama kumkimbilia yeye. "kwenda kwako kwa ulinzi"

wale wanaolipenda jina lako

Jina la Mungu linamwakilisha yeye. "wale wanaokupenda"

utawazunguka na fadhila kama ngao

Fadhila za Mungu zinazungumziwa kama ngao. "utawaonesha fadhila na kuwalinda kama askari wanavyojilina kwa ngao" au "kwa sababu u mkarimu kwao, utawalinda"

Psalms 6

Psalms 6:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

kwenye vyombo vya nyuzi

"watu wanapaswa kucheza vyombo vya nyuzi na wimbo huu"

weka kwa mtindo wa Sheminithi

Hii inaweza kumaanisha mtindo wa muziki.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

mifupa yangu inatetemeka

Mifupa inaashiria mwili wote. Mwili wake unaweza kuwa unatetemeka kwa sababu alikuwa mgonjwa au amechoka sana. "mwili wangu wote unatetemeka"

Psalms 6:3

imetaabika sana

"ogopa" au "wasiwasi"

hii itaendelea hadi lini?

Daudi anatumia swali hili kuonesha kuwa hataki kuendelea kujisikia mdhaifu na mwenye taabu. "tafadhali, usiruhusu hii iendelee!"

Rudi, Yahwe

Daudi anazungumzia Mungu kumtendea wema kama Mungu kurudi kwake. "Yahwe, rudi kwangu" au "Nione huruma, Yahwe"

Kwa kuwa katika kifo hakuna kumbukuku lako. Nani atakupa shukrani kuzimu?

Sentensi hizi mbili zina maana ya kufanana.

Kwa kuwa katika kifo hakuna kumbukuku lako.

Kumbukumbu inaashiria sifa. "Kwa kuwa watu wanapokufa, hawakusifu tena"

Nani atakupa shukrani kuzimu?

Daudi anatumia swali hili kusisitiza kuwa hakuna mtu anayetoa shukrani kwa Mungu toka kuzimu. "Hakuna mtu kuzimu atayekupa shukrani!" au "Wafu hawawezi kukusifu"

Psalms 6:6

Nimechoka na kulia kwangu kwa sauti ya kuelemewa

Kulia kwake kwa sauti ya kuelemewa inaonesha maumivu na mateso aliyoyasikia. "Nimechoka sana kwa sababu ya maumivu

ninaloanisha kitanda changu kwa machozi: ninaosha jilanza langu kwa machozi

Sentensi hizi zina maana moja.

ninaloanisha kitanda changu kwa machozi

"Ninafanya kitanda changu kilowe kwa machozi" au "Kitanda changu kimelowana kwa sababu ya machozi yangu"

ninaosha jilanza langu kwa machozi

"Nilifanya jilaza langu lilowane kwa machozi yangu"

macho yangu yanachoka

Uwezo wa kuona unazungumziwa kwa njia ya macho. "Kuona kwangu kumefifia" au "Siwezi kuona vizuri"

kutokana na huzuni

Huzuni hapa inamaanisha kulia. "kutokana na kulia" au "kwa sababu nalia sana"

Psalms 6:8

Yahwe amesikia ombi langu la huruma ... Yahwe amekubali ombi langu

Mistari hii miwili ina maana ya kufanana.

Yahwe amekubali ombi langu

Kuwa tayari kufanya ambacho Daudi ameomba inazungumziwa kama kukubali ombi lake. "Yahwe atajibu ombi langu"

Psalms 7

Psalms 7:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Utunzi wa kimuziki wa Daudi

"Huu ni wimbo ambao Daudi aliaandika"

kuhusu maneno ya Kushi Mbenyamini

Usemi "maneno ya Kushi" yanamaanisha alichosema. "kuhusu Kushi, mwanamme kutoka kabila la Benyamini alichosema"

wanaokimbia kwako

Kwenda kwa Yahwe kwa ajili ya ulinzi kunazungumziwa kama kumkimbilia. "kwenda kwako kwa ulinzi!"

watanirarua vipande vipande kama simba

Daudi anawazungumzia adui zake kumshambulia kana kwamba wanamrarua mwili wake na kumwacha vipande vipande kama simba afanyavyo. "wataniua kikatili kama simba anavyorarua mwili wa mawindo yake na kuugawa vipande vipande" au "wataniua kikatili"

bila kuwa na yeyote mwingine kuniletea mahali salama

"na hakuna mwingine atakayeweza kuniokoa"

Psalms 7:3

hakuna udhalimu mikononi mwangu

Mikono inaashiria jambo analofanya mtu. Kuwa na udhalimu juu yake inamaanisha kuwa amefanya kitu kisicho cha haki. "hakuna udhalimu ni kile nilichofanya" au "sijafanya chochote kisicho cha haki kwa yeyote"

Psalms 7:5

maisha yangu

Maisha yanaashiria mtu. "mimi"

kuyapita

"kufikia" au "kuipata." Hii inamaanisha kumshika. "kunikamata"

acha akanyage mwili wangu ulio hai ardhini

Hapa "mwili wangu ulio hai" unamaanisha mwandishi. "waruhusu adui zangu kuniangamiza"

nimelala bila heshima kwenye vumbi

Hii inamaana kulala akiwa amekufa na bila kuzikwa katika aibu.

Psalms 7:6

Inuka, Yahwe, katika hasira yako

Kuinuka inamaanisha kufanya jambo au kuchukua hatua. "Fanya jambo katika hasira yako" au "Wakasirikie adui zangu na uchukue hatua"

simama dhidi ya gadhabu ya adui zangu

Kupambana na watu kunazungumziwa kama kusimama dhidi yao. "pambana dhidi ya gadhabu ya adui zangu" au "shambulia adui zangu wenye gadhabu juu yangu"

gadhabu ya adui zangu

Gadhabu yao inaashiria mashambulizi yao. "mashambulizi ya adui zangu" au "adui zangu wanaonishambulia"

amka

Kuamka kunaashiria kuanza kufanya jambo au kuchukua hatua. "Chukua hatua" au "Fanya kitu"

kwa ajili yangu

"kunisaidia"

Mataifa yamekusanyika

Hapa neno "mataifa" linamaanisha majeshi yote yaliokusanyika kushambulia.

chukua tena nafasi yako unayostahili juu yao

Kutawala watu kunazungumziwa kama kuwa juu yao. Sehemu anayostahili Yahwe inamaanisha mojawapo kati ya mbinguni au kutawala kwa ujumla. "Tawala juu yao kutoka mbinguni" au "Tawala juu yao"

Psalms 7:8

nithibitishe

"waoneshe kuwa sina hatia"

imarisha watu wenye haki

"wafanye watu wenye haki kuwa imara" au "wafanye watu wenye haki wafanikiwe"

wewe unayechunguza mioyo na akili

Mioyo na akili zinaashiria tamaa na mawazo ya watu. "wewe unayejua mawazo yao ya ndani"

Psalms 7:10

Ngao yangu inatoka kwa Mungu

Neno "ngao" inamaanisha ulinzi wa Mungu.

Mungu anayeudhika kila siku

Ambaye Mungu anahasira naye inaweza kuelezwa vizuri. "Mungu aliye na hasira na waovu kila siku"

Psalms 7:12

Mungu atanoa upanga wake na kuandaa upinde wake kwa ajili ya mapambano

Katika mistari ya 12 na 13, Daudi anazungumzia juu ya Mungu kuamua kuwaadhibu waovu kana kwamba Mungu ni mpambanaji anayejianda kupigana dhidi yao kwa silaha. "Mungu atachukua hatua juu yao kama mpambanaji anaye noa upanga wake na kuanda upinde wake kwa ajili ya mapambano"

Psalms 7:14

yule ambaye yuko mimba na uovu ... anajifungua mipango haribifu ... anazaa uongo wenye madhara

Daudi anazungumzia vitu ambavyo mtu mwovu anafanya kama mtu mwenye mimba na uovu ndiye mtoto. "mtu mwovu. Anafanya mipango ya kuangamiza watu kusabisha uongo wenye

Mipango yake ya uharibifu yanarudia kichwa chake mwenyewe, kwa kuwa vurugu zake zinashuka chini ya kichwa chake

Uharibifu na vurugu zinazungumziwa kana kwamba zinagonga kichwa cha mtu au kumdondokea. "Mipango yake ya uharibifu inamuangamiza, kwa kuwa vurugu yake inamshambulia" au "Anapopanga kuangamiza wengine, wengine wanamuangamiza; anaposhambulia wengine, wengine wanamshambulia"

Psalms 8

Psalms 8:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika

weka kwa mtindo wa gittithi

Hii inaweza kumaanisha mtindo wa muziki.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

jina lako lililovyo tukufu duniani kote

"Jina" la Mungu linaashiria asili yake yote. "watu duniani kote wanajua kuwa wewe ni mkuu sana"

Kutoka katika midomo ya watoto na wachanga umeumba sifa

Kusababisha watoto kumsifu Mungu kunazungumziwa kana kwamba sifa ni kitu kilichoumbwa ndani ya midomo ya watoto na kufanywa kutoka nje. "Umewapa watoto na wachanga uwezo wa kukusifu"

Psalms 8:3

mbingu zako, ambazo vidole vyako

Vidole vya Mungu vinaashiria ni yeye. "mbingu ulizoumba"

binadamu ana umuhimu gani hadi umtambue, au mtu hadi umwangalie?

Misemo hii inaelezwa kwa njia ya swali kuongeza msisitizo. "Ni ajabu kuwa unawawaza watu na kuwajali!"

binadamu ... mtu

Misemo hii yote inamaanisha watu kwa ujumla.

umewavika taji la utukufu na heshima

Utukufu na heshima zinazungumziwa kana kwamba ni mataji. Maneno "utukufu" na "heshima" yanakaribiana kwa maana. "umewapa utukufu na heshima" au "umewasababisha kuwa kama wafalme"

Psalms 8:6

Unamfanya kutawala juu ya kazi yako ... umeweka vitu vyote chini ya miguu yake

Vishazi hivi viwili vinaeleza maana ya kufanana.

Unamfanya ... chini ya miguu yake

Vishazi hivi viwili vinaeleza maana ya kufanana

kazi ya mikono yako

Mikono inaashiria yale Mungu aliyoyatenda. "vitu ulivyoumba"

umeweka vitu vyote chini ya miguu yake

Kuwa na mamlaka kutawala wengine na madaraka juu ya vitu inazungumziwa kama kuwa na hivyo vitu chini ya miguu yake. Hii inamaanisha Mungu aliwapa watu mamlaka juu ya uumbaji wote. "umempa mamlaka juu ya vitu vyote"

Psalms 8:9

Jina lako limetukuka duniani kote

Kwa mshangao huu, Daudi anaonesha furaha yake na heshima yenye uoga kuhusu Mungu alivyo mkuu. "jina lako limetukuka vizuri duniani kote" au "watu duniani kote wanajua ulivyotukuka"

jina lako

"Jina" la Mungu linamaanisha yeye au sifa yake. "sifa yako"

limetukuka

"zuri" au "kuu"

Psalms 9

Psalms 9:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

weka kwa mtindo wa Muthi Labeni

Hii inaweza kumaanisha mtindo wa muziki.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Nitampa shukrani Yahwe kwa moyo wangu wote

Kwa sababu wimbo huu ameandikiwa Yahwe, Yahwe anaweza kupelekea kumita "wewe." "Yahwe, nitakupa wewe shukrani kwa moyo wangu wote"

matendo yako ya ajabu

Nomino "matendo" inaweza kuelezwa na kitenzi "kufanya." "matendo yote ya ajabu unayofanya" au "matendo yote ya ajabu uliyofanya"

Nitaimbia sifa jina lako

Hapa jina la Mungu linamaanisha ni Mungu. "Nitakuimbia sifa"

Psalms 9:3

geuka

"kurudi" au "kukimbia kwa uoga"

umeketi kwenye kiti cha enzi, hakimu mwenye haki

Wafalme walikuwa na mamlaka ya kuhukumu watu, na waliketi katika kiti cha enzi walipokuwa wakihukumu. Daudi anazungumza kana kwamba Mungu alikuwa mfalme wa kidunia. "unahukumu kama mfalme anayeketi katika kiti chake cha enzi, na u mwenye haki"

Psalms 9:5

umelifuta jina lao milele na milele

Kusababisha watu kusahaulika inazungumziwa kama kufuta jina lake. "umesababisha wasahaulike kana kwamba umefuta majina yao" au "hakuna atakaye wakumbuka tena daima"

umelifuta

"umeondoa"

Adui alivunjika kama uharibifu

Adui anazungumziwa kana kwamba alikuwa mji uliojaa majinge yaliyovunjika. "Adui zetu waliangamizwa"

ulipopindua miji yao

"Ulipoangamiza miji yao"

Kumbukumbu yao yote imepotea

Kumbukumbu inazungumziwa kana kwamba kilikuwa kiumbe hai kinachoweza kufa. "Kumbukumbu yao imesimama" au "Hakuna tena kumbukumbu yao"

Kumbukumbu yao yote imepotea

Kumbukumbu inaweza kuelezwa na kitenzi "kumbuka." "Hakuna mtu anaye wakumbuka kabisa"

Psalms 9:7

Yahwe anabaki milele

"Kubaki" inaweza kuashiria kuketi kwenye kiti cha enzi kama mfalme. "Yahwe anaketi kwenye kiti chake cha enzi milele" au "Yahwe anatawala milele"

ameweka kiti chake cha enzi kwa jili ya haki

Msemo "kiti chake cha enzi" unaashiria utawala wa Mungu. Maana zinazowezekana ni 1) "Anatawala ili ahukumu watu" au "Anatawala juu ya watu kwa haki"

Atahukumu ulimwengu kwa haki ... atatekeleza hukumu kwa ajili ya mataifa kwa kutopendelea.

Vishazi hivi viwili vinaeleza kitu kimoja.

Atahukumu ulimwengu kwa haki

Hapa "ulimwengu" unamaanisha watu wote duniani. "Atahukumu watu wote duniani kwa haki"

Psalms 9:9

Yahwe pia atakuwa ngome kwa wanaokandamizwa

Mungu anazungumziwa kana kwamba alikuwa ni sehemu ambapo watu wanaweza kwenda kwa ajili ya usalama. "Yahwe pia atawalinda wanaokandamizwa" au "Yahwe atawapa usalama wale wanaokandamizwa"

ngome

"pa kukimbila" au "kivuli"

Wale wanaolijua jina lako

Hapa maneno "jina lako" yanamaanisha Mungu. "Wale wanaokujua"

usiwatelekeze

"usiwaache"

Psalms 9:11

anaye tawala Sayuni

"anayeishi Yerusalemu"

waambie mataifa

Hapa "mataifa" yamaanisha watu wote.

Kwa kuwa Mungu anayelipiza kisasi cha damu iliyo mwagika hukumbuka

Kile anachokumbuka kinaweza kuwekwa wazi. "Kwa kuwa Mungu anaye lipiza kisasi umwagaji damu anawakumbuka wale waliouliwa" au "Kwa kuwa Mungu hukumbuka anawakumbuka wale waliouliwa na kuwaadhibu wauwaji"

hasahau kilio chao

"Anajali kilio chao"

Psalms 9:13

tazama jinsi ninavyokandamizwa na wale wanaonichukia

Hii inawezwa kuelezwa katika hali ya kutenda. "tazama wale wanaonichukia wanavyonikandamiza" au "tazama jinsi adui zangu wanavyonitendea vibaya"

wewe unayeweza kuniokoa kutoka malango ya mauti

Mauti inazungumziwa kana kwamba ni mji ulio na malango ambayo watu huingia. Kama mtu yuko karibu na malango ya mauti, inamaanisha kuwa atakufa punde. Kumzuia mtu kutokufa inazungumziwa kama kumwondoa kwenye malango ya mji. "wewe unayeweza kuniokoa na mauti" au "wewe unayeweza kuzuia nisife"

Psalms 9:15

Mataifa yamezama chini kwenye shimo walilotengeneza

Watu huchimba mashimo ili kukamata wanyama wanaoanguka humo. Hapa kuchimba shimo inaashiria kufanya mipango ya kuangamiza watu. "Mataifa ni kama watu wanaochimba mashimo kwa ajili ya wengine na kisha kuanguka humo"

miguu yao imenaswa kwenye wavu walioficha

Watu huficha nyavu ili kukamata wanyama wanaonaswa humo. Hapa kuficha wavu inaashiria kufanya mipango ya kuangamiza watu. "ni kama watu wanaoficha wavu na kunaswa humo"

ametegwa

"kunaswa" au "kushikwa." Hii inamaanisha kuangamizwa. "kuangamizwa"

Psalms 9:17

wanageuzwa

"wanakataliwa"

hatima ya mataifa yote yanayomsahau Mungu

"pale ambapo mataifa yote yanayomsahau Mungu yatakapokuwa"

Kwa kuwa wahitaji hawatasahauliwa daima

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Mungu hatawasahau wahitaji daima" au "Mungu atawakumbuka wahitaji"

wala matumaina ya waliokandamizwa kufutwa

Matumaini yanazungumziwa kana kwamba ni vitu vinavyoweza kuvunjika au kuharibika. Matumaini kuangamizwa inaashiria mambo ambayo watu wanatumaini kutokutokea. "na wanaokandamizwa hawatatumaini milele bila kuona matokeo" au "na siku moja kile wanaokandamizwa wanachotumaini kitatokea"

Psalms 9:19

Inuka

Kuinuka kunaashiria kuanza kufanya kitu. "Fanya kitu" au "Chukua hatua"

mwanadamu

"watu"

yahukumiwe

Hapa kuhukumu kunaashiria kuadhibu. "yaadhibiwe"

machoni pako

Hapa machoni inamaanisha uwepo. "katika uwepo wako"

mataifa yahukumiwe machoni pako

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "hukumu mataifa katika uwepo wako" au "yapeleke mataifa katika uwepo wako na uyaadhibu"

Psalms 10

Psalms 10:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa nini, Yahwe, unasimama mbali? Kwa nini unajificha nyakati za taabu?

Mwandishi anatumia maswali haya kuonesha huzuni yake kuwa Mungu hajamsaidia. "Yahwe, inaonekana kana kwamba uko mbali na mimi na unajificha kwangu kila ninapokuwa kwenye

njama

"mipango"

mtu mwovu

Hii inamaanisha watu waovu kwa ujumla. "watu waovu"

tamaa yake ya nafsi

Nomino "tamaa" inaweza kuelezwa na kitenzi "kutaka." "vitu anavyotaka sana kufanya"

walafi

"watu wenye tamaa"

Psalms 10:4

Mtu mwovu

Hii inamaanisha watu waovu kwa ujumla. "watu waovu"

ana uso ulioinuka

Uso ulioinuka inaashiria kiburi. "Ana tabia ya kiburi" au "ana kiburi"

hamtafuti Mungu

Kumtafuta Mungu inamaanisha kati ya 1) kumwomba Mungu msaada au 2) kumwaza Mungu na kumtii. "hamwombi Mungu msaada" au "hamwazi Mungu"

Yuko salama muda wote

Hayuko salama kweli ila anadhani yuko salama.

amri zako za haki ziko juu sana kwake

Jambo lililogumu kuelewa linazungumziwa kana kwamba liko juu sana kufikia. "hawezi kuelewa amri zako za haki"

anawakoromea adui zake

Watu hukoromea adui zao wanapodhani kuwa adui zao ni wanyonge na hawana faida. "anafikiri kuwa adui zake wote ni wanyonge na wasio na faida" au "anawakoromea adui zake wote"

anawakoromea

Hii inamaanisha kuwa anapuliza hewa kwa sauti kutoka puani mwake.

Psalms 10:6

Anasema

"Mtu mwovu anasema"

katika vizazi vyote

Hii inaweza kumaanisha "milele."

sitakutana na taabu

Kupitia taabu inazungumziwa kama kukutana nayo. "Sitakuwa na shida zozote"

Mdomo wake umejaa laana na maneno ya uongo na ya kudhuru

Kile watu wanachosema kinazungumziwa kama kuwa mdomoni mwao. "huwa anawalaani watu na kusema vitu ambavyo ni vya uongo na vya kudhuru" au "Huwa analaani watu, kusema uongo, na kutishia kuwadhuru watu"

ulimi wake huumiza na kuangamiza

Hapa ulimi unaashiria kuongea. au "kile anachokisema kinaumiza na kuangamiza watu" au "anazungumza maneno yanayowatisha na kuumiza watu"

Psalms 10:8

Anasubiri tayari kwa kuvamia

Anayesubiri ni mtu mwovu

macho yake hutafuta mhanga asiyejiweza

Macho yamamwakilisha yeye. "anatafuta mhanga asiyejiweza"

Hujificha sehemu ya siri kama simba kwenye kichaka

Hii inamzungumzia mtu mwovu kana kwamba ni simba. "Anajificha wakati akisubiri wangyonge wapite karibu yake, kama simba anavyosubiri kwa utulivu katika kichaka kwa ajili ya mnyama anayetaka kushambulia"

Hujificha

Kujificha na kusudi la kudhuru au kuua.

hulala na kusubiri

"hulala chini akisubiri" au "anajificha na kusubiri"

Anashika waliokandamizwa anapovuta wavy wake

Mwandishi anazungumzia mtu mwovu kuwashika watu kana kwamba ni mwindaji anatumia wavu kushika wanyama. "Anawashika walio kandamizwa kama mwindaji anayomshika mnywama kwenye wavu na kumvuta.

wanaanguka kwenye nyavu zake imara

Mwandishi anaendelea kumzungumzia mtu mwovu kuwashika watu kana kwamba ni mwindaji, mipango yake ni nyavu, na watu ni wanyama wanaoangukia kwenye wavu. "wahanga wake wanakamatwa na mipango yake kama wanyama wanaoanguka kwenye wavu imara wa mwindaji"

Psalms 10:11

Asema

Anayesema ni mtu mwovu na watu waovu kwa ujumla.

Mungu amesahau

Kukataa kuzingatia kile ambacho watu wanafanya inazungumziwa kama kusahau. "Mungu hazingati" au "Mungu hajali kuhusu kile nachofanya"

anafunika uso wake

Kukataa kuzingatia kitu ambacho mtu anafanya kama kufunika uso wa mtu. "Mungu anakataa kuona kinachotokea"

hatahangaika kutazama

Kuzingatia kile ambacho mtu anafanya inazungumziwa kama kukiangalia. "hatahangaika kuzingatia" au "hatajali"

Inuka

Kuanza kufanya kitu inazungumziwa kama kuinuka. "Fanya kitu"

Inua mkono wako

Hapa kuinua mkono kumpiga mtu inaashiria kumwadhibu. "kumpiga kwa nguvu" au "kumwadhibu mtu mwovu"

Psalms 10:13

Kwa nini mtu mwovu anamkataa Mungu na kusema ... "Hutaniwajibisha"?

Mwandishi anatumia swali hili kuonesha kuwa anachosema ni cha kusikitisha sana kuwa watu waovu wanafanya vitu hivi. "Watu waovu humktaa Mungu kila wakati na kusema .. 'Hautaniwajisbisha.'"

Hutaniwajibisha

"Hutaniomba kukueleza kwa nini ninafanya ninachokifanya." Kumwajibisha mtu hapa inaashiria kumwadhibu. "Hautaniadhibu"

Psalms 10:15

Kuvunja mkono wa mwovu na mtu mbaya

Hapa "mkono" unaashiria nguvu. "Kuangamiza nguvu ya mwovu na mtu mbaya" au "Kumfanya mtu mwovu na mbaya kuwa mnyonge"

mwovu na mtu mbaya

Maneno haya yana maana sawa.

Kumfanya awajibike kwa matendo yake maovu

Kumfanya mtu awajibike kwa matendo yake maovu inaashiria kumwadhibu. "Muadhibu kwa mambo maovu aliyotenda"

mataifa yanatolewa kwenye nchi yake

"Yahwe anawalazimisha watu wa mataifa kuondoka nchini kwake"

Psalms 10:17

umesikia mahitaji ya wanao kandamizwa

Inaonesha kuwa watu wanao kandamizwa walilia kwa Mungu. "watu wanao kandamizwa wakilia kwako, uliwasikiliza wakikuambia walichohitaji"

unautia nguvu moyo wao

Moyo imara inaashiria ujasiri, na kufanya mioyo ya watu kuwa imara inaashiria kuwatia moyo. "unawatia moyo" au "unawafanya kujiamini"

hakuna mtu ... atakaye sababisha hofu tena

"hakuna mtu ... atakaye sababisha watu kuogopa tena"

Psalms 11

Psalms 11:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

ninamkimbilia Yahwe

Kwenda kwa Yahwe kwa ajili ya ulinzi kunazungumziwa kama kumkimbilia. "kwenda kwa Yahwe kwa ulinzi"

utasemaje kwangu, "Kimbia kama ndege milimani?"

Swali hili linaulizwa kutoa msisitizo. Linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Kwa hiyo usiniambie kukimbia!"

Maana tazama! Waovu wanaanda upinde wao. Wanafanya tayari mishale yao kwenye nyuzi kupiga gizani kwa wanyofu moyoni.

"Tazama! waovu wanajiandaa kuvamia watu wanyofu"

wanyofu moyoni

Hapa "wanyofu moyoni" inamaanisha watu wanaomcha Mungu au wenye haki.

Psalms 11:3

Maana misingi imeharibika, mwenye haki atafanya nini?

Hapa "misingi" inaweza kumaanisha sheria na utaratibu. Swali hili la balagha linaulizwa kuongeza msisitizo. Linaweza kutafsiririwa kama kauli. "Watu wenye haki hawawezi kufanya lolote pale watu waovu wasipoadhibiwa wanapokeuka sheria!"

Macho yake yanatazama, macho yake yanachunguza watoto wa binadamu

Yahwe anajua kila kitu kinachotokea. "Anachunguza yote wanayofanya wanadamu"

watoto wa binadamu

"wanadamu"

Psalms 11:5

anachunguza

"kuangalia kwa umakini"

wanaofanya fujo

"kuumiza wengine"

Anawanyeshea moto wa makaa na kibiriti juu ya waovu; upepo unaochoma utakua sehemu yao kutoka kwenye kikombe chake!

Adhabu ya Mungu inaelezwa kana kwamba yalikuwa makaa ya moto na kibiriti kutoka kwenye volkano. "Anawaadhibu waovu; hakutakuwa na nafuu kwao!"

kibiriti

Hili ni jina lingine la salfa

wataona uso wake

"kuwa kwenye uwepo wake"

Psalms 12

Psalms 12:1

Taarifa ya Jumla:

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

weka kwa mtindo wa Sheminithi

Hii inaweza kumaanisha mtindo wa muziki.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Nisaidie, Yahwe

"Yahwe, njoo unisaidie"

waaminifu wamepotea

"watu waaminifu wamepotea wote"

Psalms 12:2

Kila mmjoa anasema ... kila mmoja anazungumza

Kurudiwa mara mbili kwa "kila mmoja" ni kukuza maneno, yanatumika kusisitiza kuwa tatizo lilikuwa kubwa.

midomo ya

"sifa ya uongo"

moyo mara mbili

"maneno yanayopotosha"

kata midomo yote ya kujipendekeza

"wazuie kuzungumza sifa za uongo"

kila ulimi unaotangaza mambo makuu

Hapa "ulimi" unaashiria maneno ya kujidai. "kila mtu anayejidai"

Kwa ndimi zetu tutashinda

Hapa maneno "ndimi zetu" yanamaanisha maneno mengi wanayoyazungumza. "Kuzungumza maneno mengi kutatufanya washindi"

tutashinda

"tutafanikiwa"

nani anaweza kuwa mkuu juu yetu?

Hili swali la balagha linaulizwa kusisitiza kuwa waliamini kuwa hakuna anayeweza kuwatala. Inaweza kutafsiriwa kama kauli. "hakuna anayeweza kutawala juu yetu!"

Psalms 12:5

mgumio

Hizi ni sauti nzito ambazo watu hufanya kwa sababu ya maumivu au hisia kali

nitainuka," asema Yahwe

Hii inamaanisha Yahwe atatenda kitu kuwasaidia watu.

Psalms 12:6

kama shaba iliyosafishwa kwenye tanuu duniani, kusafishwa mara saba

Maneno ya Yahwe yanalinganizhwa na shaba iliyosafishwa. "wako bila kasoro"

Unawatunza

"Unawatunza watu wenye haki"

wanatembea kila upande

"wametuzunguka"

wakati uovu unapotukuzwa miongoni mwa watoto wa wanadamu

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "wakati watu kila sehemu wanasifu uovu"

watoto wa wanadamu

"binadamu" au "watu"

Psalms 13

Psalms 13:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Hadi lini, Yahwe, utakuwa ukinisahau?

Swali hili linaulizwa kushika ufahamu wa msomaji na kuongeza msisitizo. Linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Yahwe, inaonekana kuwa umenisahau!

Hadi lini ... uso wako kwangu?

Maneno "uso wako" yanaashiria Mungu kamili. Swali hili balagha linaulizwa kuongeza msisitizo. Linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Inaonekana unajificha kwangu!"

Hadi lini adui yangu atashinda juu yangu?

Swali hili la balagha linaulizwa kuongeza msisitizo. Linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Hakika adui zangu hawatanishinda daima!"

Psalms 13:3

Nitazame na unijibu

"Nizingatie na unisikilize"

Nipe mwanga machoni mwangu

Hii ni njia ya kuomba nguvu. "Nifanye kuwa na nguvu tena"

au nitalala kifoni

"Kulala kifoni" inamaanisha kufa.

Usimruhusu adui yangu aseme ... ili adui yangu asiseme

"Usimruhusu adui yangu aseme kunihusu ... ili adui yangu asiseme kunihusu"

ninapoletwa chini

"ninapoanguka" au "wanaponishinda"

Psalms 13:5

Nimetumaini katika uaminifu wako wa agano

Kwa kuzungumzia uaminifu wa Yahwe wa agano, Daudi anatumaini kuwa Yahwe atampenda daima. "Nina imani kuwa utanipenda kwa uaminifu"

moyo wangu unafuahi ndani ya wokovu wako

Hapa "moyo wangu" unaashiria mtu mzima. "Nitafurahi kwa sababu umeniokoa"

Psalms 14

Psalms 14:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Mpumbavu husema moyoni mwake

Hii ni lahaja inayomaanisha kuzungumza mwenyewe au kujiwazia mwenyewe. "Mtu mpumbavu anajiambia"

Wameharibika

walioharibika inaashiria binadamu wapumbavu wanaosema hakuna Mungu.

Psalms 14:2

watoto wa wanadamu

Msemo huu unamaanisha wanadamu wote.

wanaonitafuta

Hii inafafanua wote wanaotamani kumjua Mungu kana kwamba walikuwa wanamfuata kabisa kwenye njia. "wanaotamani kumjua"

Wote wamegeuka

Hii inaelezea watu waliomkataa Mungu kana kwamba waliacha kutembea kwenye njia sahihi na wameenda upande mwingine. "Wote wamemgeuka Yahwe"

Psalms 14:4

Kwani hawajui chochote ... ambao hawamwiti Yahwe?

Swali hili la balagha linaulizwa kuongeza msisitizo. Linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Wanatenda kana kwamba hawajui chochote ... wasiomwita Yahwe. Lakini wanajua wanachokifanya!"

wale wanaotenda udhalimu

Hapa "udhalimu" unamaanisha matendo maovu. "wale wwnye tabia mbovu.

wale wanaowala watu wangu

Hii inamaanisha wale wanaofanya vitu viovu na wanawaangamiza watu wa Mungu kana kwamba wanakula chakula.

Psalms 14:5

Wanatemeka

Wanaotetemeke ni wale wanaotenda maovu.

Mungu yuko pamoja na mkusanyiko wa wenye haki

Kusema kuwa "Mungu yuko pamoja" na mkusanyiko wa wenye haki inamaanisha kuwa atawasaidia. HIi inaweza kuwekwa wazi. "Mungu huwasaidia wale wanaotenda haki" au "Mungu anawasaidia wale wanaotenda yaliyo sawa"

Mnataka

Wanaotaka ni watu waovu.

kumwaibishi mtu maskini

"kumfanya mtu aliye maskini kuona aibu"

Yahwe ni kimbilio lake

Hii inazungumzia ulinzi ambao Yahwe anatoa kana kwamba ulikuwa kivuli ambacho mtu atatufuta wakati wa dhoruba. "Yahwe ni kama kivuli cha ulinzi kwake"

Psalms 14:7

O, wokovu wa Israeli utatoka Sayuni

Mwandishi anasema kuwa anatamani Mungu aje kutoka Yerusalemu kuisaidia Israeli. "Ninatamani kwamba Yahwe aje kutoka Yerusalemu na kuwasaidia watu wake!"

kisha Yakobo atashangilia na Israeli kufurahi

Misemo hii miwili ina maana moja. Hapa "Yakobo na"Israeli" inawakilisha watu wa Israeli. "kisha watu wote wa Israeli watafurahi sana"

Psalms 15

Psalms 15:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Nani aishi kwenye kilima chako kitakatifu?

"Kilima kitakatifu" hapa kinaashiria hekalu la Mungu, ambalo lilikuwa kwenye mlima Sayuni. "Nani aishi kwenye sehemu yako takatifu?"

anazungumza ukweli kutoka moyoni mwake

"anazungumza ukweli"

Psalms 15:3

Hakashifu

Hii inaashiria mtu mwenye haki katika 15:1.

Hakashifu kwa ulimi wake

Hapa "ulimi" unaashiria maneno maovu. "Hasemi mambo maovu kuhusu watu wasio na hatia"

Hadhuru

"kuumiza" au "kuharibu"

Psalms 15:4

Mtu asiyefaa ni chukizo machoni pake, lakini anawaheshimu wale wanaomcha Yahwe

"Watu wenye haki wanachukia wale waliomkataa Mungu, lakini wanawaheshimu wale wanaomheshimu Mungu"

Mtu asiyefaa

"Mtu mwovu" au"Mtu aliyemkataa Yahwe"

hatatikisika

Hapa "kutikisika" kunaashiria kutokuishi kwa usalama tena. Hii inaweza kuelezwa katika hali chanya. "wataishi katia usalama"

Psalms 16

Psalms 16:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Daudi

Hii inaweza kuandikwa kama: "Hii ni zaburi ambayo Daudi aliandika."

kukimbilia wewe

Kwenda kwa Yahwe kwa ajili ya ulinzi inazungumziwa kama kumkimbilia yeye. "kwenda kwako kwa jili ya ulinzi"

watu watakatifu waliomo duniani

Hapa "watu watakatifu" inaashiria watu wa Mungu wanaomuamini. "watu wako wanaoishi katika nchi hii"

Psalms 16:4

Taabu zao zita... miungu

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Taabu za wale wanaotafuta miungu mingine zitaongezeka"

sitamwaga ... damu kwa miungu wao

"kutoa sadaka kwa miungu yao"

kuinua majina yao na midomo yangu

Kuinua "majina yao na midomo yangu" inamaanisha kusifu miungu mingine au kuomba kwao.

Psalms 16:5

sehemu yangu niliyochagua

Hapa Daudi anamzungumzia Yahwe kana kwamba alikuwa ni sehemu ya nchi ambayo alipewa.

kikombe changu

Hapa Daudi anamzungumzia Yahwe kana kwamba alikuwa ni kikombe chenye baraka nyingi. "ambaye hunibariki"

Unashikilia hatima yangu

"Unaamua siku zangu za usoni"

Kamba za kupima ... katika sehemu nzuri

Baraka za Mungu kwa Daudi zinazungumziwa kana kwamba ni sehemu ya nchi iliyochunguzwa kwa jili yake kumiliki. "Kamba za kupima" zinaashiria kamba za mchunguzi wa ardhi. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Sehemu uliyonipa inapendeza"

hakika urithi wa kupendeza ni wangu

Hapa Daudi anazungumzia baraka za Yahwe kana kwamba zilikuwa ni urithi ambao alipokea. "Nimefurahi kwa vitu vyote alivyonipa"

Psalms 16:7

Nimemuweka Yahwe mbele yangu muda wote

"Daima nakumbuka kuwa Yahwe yuko pamoja na mimi"

ili nisitikiswe kutoka mkono wake wa kuume

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "hakuna kitu kitakachonitoa upande wake"

Psalms 16:9

Taarifa ya Jumla:

Daudi anaendelea kuzungumza na Mungu.

Kwa hiyo moyo wangu una furaha; utukufu wangu unashangilia

Msemaji anasema kwamba kuweza kumsifu Mungu kunamletea yeye heshima. Vishazi hivi viwili vinaeleza vitu vya kufanana. "Kwa hiyo nina furaha, nina heshima kumsifu"

moyo wangu

Hapa "moyo" unaashiria mawazo na hisia za msemaji.

utukufu wangu

Matoleo mengi yanatafsiri "utukufu wangu" kumaanisha moyo wa mwandishi, anayekuwa na heshima kushangilia kwa sababu ya Mungu.

Psalms 16:11

tele

"kubwa" au "kiasi kikubwa cha"

furaha ... inakaa katika uwepo wako

Mwandishi anazungumzia "furaha" kana kwamba ni mtu.

katika mkono wako wa kuume

Maneno "mkono wako wa kuume" yanaonesha kuwa katika uwepo maalum wa Mungu. "Ninapokuwa karibu na wewe"

Psalms 17

Psalms 17:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Ombi la Daudi

"Hili ni ombi ambalo Daudi aliaandika."

Nipe sikio ombi langu kutoka midomo isiyo na uongo

Msemo "nipe sikio" unamaanisha kusikiliza, na neno "midomo" inaashiria maneno ambayo mtu huongea. "Sikiliza ombi langu ambalo halitoki katika midomo ya uongo"

Acha uthibitisho wangu uje kutoka katika uwepo wako

Hapa "uwepo" inaashiria Yahwe. "Nitamke kuwa sina hatia"

acha macho yako yaone kilicho sawa!

Hapa "macho yako" inaashiria kile ambacho Yahwe anajua kuwa kweli. "unajua kuwa ninakuambia ukweli!"

Psalms 17:3

Ukiujaribu moyo wangu, ukija kwangu usiku

Hapa " ukiujaribu moyo wangu" inamaansiha kupima mawazo na nia. "ukipima mawazo yangu usiku"

mdomo wangu hutatenda dhambi

Hapa mdomo unazungumziwa kana kwamba unaweza kutenda wenyewe. Pia inawakilisha maneno ambayo mtu huzungumza. "Sitasema uongo au kutenda dhambi kwa maneo yangu

Psalms 17:4

ni kwa neno la midomo yako nimetunza kutoka katika njia za wahalifu

Hapa "neno la midomo yako" inamaanisha maelekezo ya Mungu. "maelekezo yako yamenisabisha kuepuka kufanya mambo maovu"

Hatua zangu zimeshikilia kwa nguvu kwenye njia zako; miguu yangu yaijateleza

Vishazi hivi viwili vinamaanisha kitu kimoja. Kurudia kunaongeza msisitizo.

miguu yangu yaijateleza

Mwandishi anazungumzia kumtii Mungu kana kwamba anatembea katika mjia. "nimedhamiria kufuata njia zako"

Psalms 17:6

geuza sikio lako kwangu ... sikiliza ninapozungumza

Misemo hii miwili ina maana sawa. Hapa "sikio lako" linamaanisha utayari wa Mungu kumsikiliza mtu anayemuomba. "nizingatie ... nisikilize ninapozungumza"

mkono wako wa kuume

"Mkono wa kuume" unaashiria nguvu ya Mungu. "uwezo wako mkuu"

kukimbilia

Kwenda kwa Yahwe kwa ajili ya ulinzi inazungumziwa kama kumkimbilia. "kwenda kwako kwa ajili ya ulinzi"

Psalms 17:8

Nilinde kama mboni la jicho lako

"mboni la jicho lako" inaashiria kitu kilicho na thamani. "Nilinde kama utakavyolinda kitu cha thamani sana"

nifiche chini ya kivuli cha mbawa zako

Daudi anazungumzia ulinzi wa Mungu kana kwamba alikuwa ni ndege anayelinda watoto wake chini ya mbawa zake. "Niweke salama kama ndege anavyolinda makinda yake chini ya mbawa zake"

midomo yao inazungumza kwa majivuno

Hapa "midomo yao inazungumza" inamaanisha kile ambacho watu wanasema. "huwa wanajidai"

Psalms 17:11

Wamezunguka hatua zangu

Hapa "wamezunguka hatua zangu" inaashiria jinsi adui wa Daudi walivyomfuata kila mahali ili kumkamata. "Adui zangu wamenizunguka"

kama simba mwenye hamu kwa ajili ya mhanga, kama simba mchanga aliyejikunyata katika maficho

Misemo hii miwili inaonesha mawazo ya kufanana. Kurudia kunaongeza mkazo.

Wao ni kama simba ... kama simba mchanga

Mwandishi inahisi kufuatiliwa kama simba anavyowinda windo lake.

Psalms 17:13

Okoa maisha yangu kutoka kwa mwovu kwa upanga wako ... Niokoe kutoka kwa watu kwa mkono wako, Yahwe, kutoka kwa wanaume wa dunia hii

Vishazi hivi viwili vina maana ya kufanana. Kurudiwa kunaongeza mkazo wa maneno ya mwandishi.

kwa upanga wako ... kwa mkono wako

Hapa "upanga" na "mkono" yote inaashiria nguvu ya Yahwe.

Utajaza matumbo ya hazina yako na utajiri

Maandiko ya zamani yanapotosha. Maana zinazowezekana ni 1) Yahwe atatoa baraka nyingi kwa watu wake. "Utawabariki watu wako sana" au 2) Yahwe atawaadhibu kwa nguvu watu waovu hadi watoto na wajukuu wao.

Psalms 17:15

Nitauona uso wako katika haki

Hapa "uso" unamwakilisha Yahwe. Daudi anaujasiri kuwa atamuona Yahwe. "kwa sababu ninatenda yaliyo sawa, nitakuwa na wewe siku moja"

Nitaridhika nitakapoamka, na kukutazama wewe

Daudi anaamini kuwa baada ya kufa, atakuwa na Yahwe. Hii naweza kuweka wazi. "Baada ya kufa, nitafurahi kuamka katika uwepo wako"

Psalms 18

Psalms 18:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

akamwimbia Yahwe maneno ya wimbo huu

"aliimba wimbo huu kwa Yahwe"

katika siku ambayo Yahwe aliniokoa

"baada ya Yahwe kumwokoa"

kutoka katika mkono wa Sauli

Hapa "mkono" unamaanisha nguvu ya Sauli. "kutoka katika nguvu ya Sauli"

Psalms 18:2

Yahwe ni mwamba wangu

Daudi anamzungumzia Yahwe kana kwamba ni mwamba. Neno "mwamba" ni picha ya sehemu salama.

mwamba wangu, boma langu

Hapa maneno "mwamba" na "boma" zinamaana ya kufanana na zinasisitiza kuwa Yahwe anatoa usalama kutoka kwa adui.

mkimbilia

Kwenda kwa Yahwe kwa ajili ya ulinzi kunazungumziwa kama kumkimbilia. "kwenda kwake kwa ajili ya ulinzi"

ngao yangu, pembe la wokovu wangu, na ngome yangu

Daudi anamzungumzia Yahwe kana kwamba ni "ngao," "pembe" la wokovu, na "ngome" yake. Yahwe ndiye anayemlinda na mabaya. Hapa wazo la kufanana linarudiwa kwa njia tatu kwa ajili ya mkazo.

Nitaokolewa kutoka kwa adui zangu

"Nitaokolewa kutoka kwa adui zangu"

Psalms 18:4

Kamba za mauti zinanizunguka

Daudi anazungumzia kifo kana kwamba ni mtu anayeweza kukamata na kumfunga kwa kamba. "Nilikuwa nataka kuuwawa"

maji yanayokimbia ya yasiyofaa

Daudi ni mnyonge kana kwamba anabebwa na mafuriko ya maji yanayokimbia. "Nilihisi kuwa mnyonge kabisa"

Kamba za kuzimu zinanizunguka; mitego ya mauti imeninasa

Hapa "kuzimu," sehemu ya wafu, na "mauti" zinazungumziwa kana kwamba ni watu wanaoweza kumzunguka na kumtega. Vishazi hivi viwili vina maana ya kufanana na wazo linarudiwa kwa ajili ya mkazo. "Nilihisi kubanwa na nikadhani ninaenda kufa"

Psalms 18:6

Katika huzuni yangu

"katika hitaji langu kubwa" au "katika kukata tamaa kwangu"

kilio changu kikaenda katika uwepo wake

Hapa Daudi anazungumzia "kilio" chake kana kwamba ni mtu anayeweza kuja katika uwepo wa Yahwe. "Nikamuomba"

kikaenda katika maskio yake

Hapa Daudi anazungumzia jinsi Yahwe alivyosikia kilio chake cha msaada. Wazo linarudiwa kwa ajili ya mkazo. "akasikia maombi yangu"

Psalms 18:7

Kisha ulimwengu ... ikatikiswa kwa sababu Mungu alikuwa na hasira

Mungu kuwa na hasira inazungumziwa kana kwamba ilikuwa ni tetemeko baya. "Mungu alikuwa na hasira sana hadi ikawa kama dunia ... ikatikisika"

ulimwengu ukatikisika na kutetemeka

Maneno "kutikisika" na "kutetemeka" yana maana sawa na yanasisitiza jinsi dunia ilivyotikisika. "nchi ikasogea huku na kule" au "ardhi ikasogea juu na chini" au "kulikuwa na tetemeko kali"

misingi ya milima pia ikatetemeka na kutikiswa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "misingi ya milima pia ikatetemeka na kutikisika"

Moshi ukatoka kwenye tundu zake za pua ... Makaa ikawashwa nao

Daudi anamzungumzia Yahwe kana kwamba alikuwa akipumua moto. Hii ni picha ya jinsi Mungu alivyokasirika.

moto ukatoka mdomoni mwake. Makaa ikawashwa nao.

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "moto ukatoka katika mdomo wake na kuwasha makaa"

Psalms 18:9

Akafungua

Aliyefungua ni Yahwe.

giza nene lilikuwa chini ya miguu yake

Ingawa Yahwe sio binadamu, mwandishi anampa sifa za binadamu. "giza nene lilikuwa chini yake"

mabawa ya upepo

Hapa mwandishi wa zaburi anazungumzia upepo kana kwamba una mabawa kama malaika.

Psalms 18:11

Akafanya giza ... yeye

Hapa neno "yeye" linamaanisha Yahwe

Akafanya giza hema

Hapa giza linazungumziwa kana kwamba ni hema. "Akafanya giza kitu cha kufunikia" au "Akafanya giza sehemu ya kujifichia"

mawingu mazito ya mvua

"mawingu na mvua kubwa" au "mawingu manene, meusi"

Mvua ya mawe

"mawe ya barafu"

Psalms 18:13

Yahwe akaunguruma mbinguni

Sauti ya Yahwe ilikuwa kama ya radi

Aliye juu

"Aliye juu" inamaanisha Yahwe.

Akapiga mishale yake na kuwatawanya adui zake ... miale ya radi ikawatawanyisha

Vishazi hivi viwili vina maana ya kukaribiana.

Akapiga mishale yake na kuwatawanya adui zake

Hapa miale ya radi inazungumziwa kana kwamba ni mishale.

ikawatawanyisha

"ikawapeleka pande tofauti"

Psalms 18:15

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaendelea kuzungumzia uwezo wa Yahwe.

Kisha mikondo ya maji ikatokea; misingi ya dunia ikawekwa wazi.

Vishazi hivi viwili vina maana ya kukaribiana. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Kisha mikondo ya maji ikatokeza na chini ya bahari pakaonekana; ukaweka wazi misingi ya dunia"

kwa mlipuko wa pumzi wa tundu zako za pua

Ingawa Mungu hana sifa za kimwili kama za binadamu zilizoelezwa hapa, picha hii inaonesha uwezo wake mkuu. Upepo unazungumziwa kana kwamba ulikuja kama mlipuko mkubwa kutoka katika tundu za pua za Mungu.

Psalms 18:16

Akafika chini ... akanishika ...Akanivuta

Anayezungumziwa hapa ni Yahwe.

maji yaliyokuwa yakienda mbele

Hapa mwandishi wa zaburi anazungumzia hatari ya adui zake kana kwamba walikuwa mawimbi makubwa au maji ya nguvu, ambapo Yahwe alimwokoa.

Psalms 18:18

Wakaja dhidi yangu

Wanazungumziwa ni adui wenye nguvu katika msatari wa 17.

Wakaja dhidi yangu katika siku ya dhiki yangu lakini Yahwe alikuwa msaada wangu

Neno "dhiki" linaeleza hali ya mtu mwenye shida nyingi. "Adui wenye nguvu walinivamia katika siku niliyokuwa na taabu nyingi, lakini Yahwe alinilinda"

Psalms 18:20

mikono yangu ilikuwa misafi

Hapa kuwa na "mikono misafi" inamaanisha mtu hana hatia. "matendo yangu yote yalikuwa sawa"

Nimetunza njia za Yahwe

Sheria za Yahwe zinazungumziwa kana kwamba zilikuwa njia ambazo mtu anapaswa kutembea. "Nimetii sheria za Yahwe"

sijageuka kwa uovu kutoka njia ya Mungu

Hapa kuwa mwovu inazungumziwa kama mtu kuacha njia sahihi na kufuata njia isiyo sahihi. "sijafanya uovu kwa kugeuka kutoka kwa Mungu wangu"

Psalms 18:22

Kwa amri zake zote za haki ... sijazigeuka

Vishazi hivi viwili vina maana ya kufanana. Mwandishi anarudia mawazo haya kwa ajili ya mkazo.

zimekuwa mbele yangu

"zimeniongoza" au "nimezikumbuka"

Pia nimekuwa bila hatia ... nimejitenga na dhambi

Vishazi hivi viwili vina maana ya kufanana. Mwandishi anarudia mawazo haya kwa ajili ya mkazo.

bila hatia mbele yake

"bila hatia kulingana na yeye"

nimejitenga na dhambi

"sijatenda dhambi"

mikono yangu ilikuwa misafi

Kuwa na "mikono misafi" inamaanisha kuwa mtu hana hatia na kosa. "matendo yangu yote yalikuwa sawa"

mbele ya macho yake

Hii inamaanisha uwepo wa Mungu. "mbele yake" au "kulingana na yeye"

Psalms 18:25

Taarifa ya

Mwandishi anazungumza na Yahwe

Kwa yeyote aliye mwaminifu

Hapa "mwaminifu" inamaanisha kufanya kile ambacho Mungu anamuamuru mtu kufanya. "kwa wale walio wanaotii kwa uaminifu amri zako" au "kwa wale wanaofanya agano lako kwa uaminifu"

kwa mwanamme asiye na lawama ... ujioneshe msafi

Vishazi hivi viwili vina maana ya kufanana. Mwandishi anarudi mawazo haya kwa ajili ya mkazo.

una akili kwa yeyote aliye mkaidi

"Unamshinda kwa akili yeyote asiye wazi"

Psalms 18:27

unawaleta chini

"unawanyenyekesha"

wenye macho ya majivuno yaliyoinuka

lahaja hii inaashiria wale walio na majivuno. "wenye majivuno"

Kwa kuwa unaipa nuru taa yangu; Yahwe Mungu wangu huipa nuru giza langu

Mwandishi anazungumzia uwepo wa Yahwe kana kwamba alikuwa nuru. Vishazi hivi vina maana ya kukaribiana.

Kwako ninaweza kuruka kizuizi

"Kwa msaada wako ninaweza kuvuka kikwazo chochote"

Psalms 18:30

Yeye ni ngao kwa kila mmoja anaye

Ngao humlinda askari. Daudi anazungumza kana kwamba Mungu alikuwa ni ngao inayomlinda. "Wewe, Yahwe, unamlinda kila mtu anayekukimbilia wewe kama kimbilio"

Kwa kuwa ni nani Mungu ila Yahwe? Nani ni mwamba ila Mungu wetu?

Jibu linalodokezwa ni hakuna mtu. "Yahwe pekee ndiye Mungu! Mungu wetu pekee ndiye mwamba!"

mwamba

Daudi anamzungumzia Yahwe kana kwamba ni mwamba anaoweza kupanda kuwatoroka adui zake.

anayeniwekea nguvu juu yangu kama mshipi

Mungu anampa nguvu Daudi kana kwamba ilikuwa ni kipande cha nguo.

anayemuweka mtu asiye na lawama katika njia yake

Hapa Daudi anazungumzia kuishi maisha yanaompendeza Mungu kana kwamba ni kuwa katika njia sahihi. "humsababisha mtu asiye na lawama kuishi maisha ya haki"

Psalms 18:33

hufanya miguu yangu miepesi

Hii inaashiria kumwezesha mtu kukimbia haraka zaidi. "hunifanya nikimbie haraka sana"

kama mbawala na kuniweka pa juu

Mbawala ana kasi na mtulivu milimani.

hufunza mikono yangu

Hapa "mikono yangu" inamaanisha mtu. "Hunifunza"

mikono yangu

Hii inaashiria mtu. "mimi"

Psalms 18:35

ngao ya wokovu wako

Hapa mwandishi anazungumzia ulinzi wa Mungu kana kwamba ni ngao. Nomino dhahania ya "wokovu" inaweza kuelezwa kama kitenzi "okoa." "ulinzi wako na kuniokoa"

Mkono wako wa kuume ... fadhili zako

Zote hizi ni njia zingine za kumwakilisha Mungu mwenyewe.

sehemu pana kwa ajili ya miguu yangu chini yangu

Mwandishi anazungumzia ulinzi ambao Mungu ameutoa kana kwamba ni eneo pana kwa ajili yake kusimama. "sehemu salama kwa ajili yangu"

miguu yangu haijateleza

Hapa "miguu yangu" inamaanisha mtu mwenyewe. Mwandishi anazungumzia usalama wa ulinzi wa Mungu kana kwamba alikuwa akisimama mahali ambapo hawezi kuteleza wala kuanguka. "Sijateleza" au "Niko salama"

Psalms 18:37

Nimewaponda

"Nimewavunja vipande vipande"

hawakuweza kuinuka

"hawakuweza kusimama"

wameanguka chini ya miguu yangu

Lahaja hii inamaansiha kuwa mwandishi wa zaburi amewashinda adui zake. "nimewashinda wote"

umeweka nguvu juu yangu kama mshipi

Mwandishi wa zaburi anasema kuwa Yahwe amempa nguvu inayomzunguka na kumstahimili kama mshipi.

umewaweka chini yangu

Hapa mwandishi wa zaburi anazungumzia kushindwa kwa adui zake kama kusimama juu yao. "unawashinda kwa ajili yangu"

wale wanaojiinua dhidi yangu

Hii inamaansiha wale wanaompinga mwandishi wa zaburi. "wale ambao ni adui zangu"

Psalms 18:40

sehemu za nyuma za shingo za adui zangu

Hii inaashiria ushindi juuya maadui wa mtu. "ushindi juu ya adui zangu"

Nimewaangamiza wale wanaonichukia

"Niliwashinda wale walionichukia" au "Niliwaangamiza kabisa wale walionichukia"

lakini hakuwajibu

Hii inamaanisha Yahwe hakutoa msaada wowote. "lakini hakuwasaidia"

Niliwapiga hadi vipande kama vumbi mbele ya upepo

Adui wa mwandishi wa zaburi wanalinganishwa na vumbi kuonesha jinsi alivyowashinda.

Nikawarusha nje kama tope katika mitaa

Adui wa mwandishi wa zaburi wanalinganishwa na tope la kwenye mitaa kuonesha jinsi alivyowashinda.

Psalms 18:43

mabishano

"kutokuelewana"

umenifanya kichwa juu ya mataifa

Hapa "kichwa" kinamaanisha mtawala. "umeniweka mimi kuwa mtawala juu ya mataifa

wageni walilazimika kusujudu

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Mungu aliwalazimisha wageni kusujudu"

wageni walikuja wakitetemeka

hapa "kutetemeka" inaonesha kuwa walikuwa wanaogopa sana. "wageni walikuja wakitetemeka, wakionesha kuwa walikuwa wanaogopa sana"

Psalms 18:46

na mwamba wangu usifiwe

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "yeye ni mwamba wangu na anapaswa kusifiwa" au "watu wasifu mwamba wangu"

mwamba wangu

Hapa mwandishi anazungumzia ulinzi wa Yahwe kana kwamba alikuwa ni mwamba uliozuia adui zake kumfikia.

Na Mungu wa wokovu wangu ainuliwe

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Na watu wamtukuze Mungu wa wokovu wangu"

Mungu wa wokovu wangu

Hii inamaanisha kuwa Mungu amemuokoa. "Mungu aliyeniokoa"

Mungu anayetekeleza kisasi kwa ajili yangu

"Kutekeleza kisasi" inamaana kuwaadhibu watu kwa matendo yao maovu. "Mungu anayewaadhibu watu kwa matendo maovu waliyotenda kwangu"

Psalms 18:48

Nimewekwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Mungu ameniweka

umeniinua

Ulinzi wa Yahwe kwa mwandishi unazungumziwa kana kwamba amemuinua mwandishi juu sana hadi adui zake hawakuweza kumfikia na kumdhuru. "umeniweka sehemu salama juu"

walioinuka dhidi yangu

"walionivamia" au "walioasi dhidi

wanaume wenye vurugu

"wanaume wakatili" au "watu wenye hasira sana"

miongoni mwa

Hapa mwandishi anamaana kuwa atampa Yahwe shukrani ili watu wote wasikie ukuu wa Yahwe. "ili mataifa yote yasikie kuhusu hili"

kwa jina lako

Hapa "jina" linamwakilisha Mungu mwenyewe. "kwa heshima ya jina lako" au "kwako"

Psalms 18:50

ushindi kwa mfalme wake

Kwa kutumia maneno "mfalme wake," Daudi anamaanisha yeye mwenyewe kama mfalme.

anaonesha uaminifu wake wa agano kwa mtiwa mafuta wake ... kwa vizazi vyake milele

"ananipenda kwa uaminifu kama alivyoahidi katika agano lake, na ataupenda uzao wangu milele"

Psalms 19

Psalms 19:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Mbingu zinatangaza

Mbingu zinaelezwa kana kwamba ni mtu. "Mbingu zinaonesha" au "Mbingu zinaonekana kama zinatangaza"

anga zinafanya kazi yake ya mikono kujulikana

Anga zinaelezwa kana kwamba ni mwalimu. "anga zinaonekana kufanya kazi ya mikono ya Mungu kujulikana kwetu"

kazi yake ya mikono

"uumbaji wake" au "ulimwengu alioutengeneza"

maneno humwagika

Kilicho kizuri kuhusu uumbaji kinafananishwa na kuzungumza, kana kwamba uumbaji ni mtu. Kisha maneno hayo yanalinganishwa na maji wanayotiririka kila mahali. "Uumbaji ni kama mtu anayezungumza na kila mtu"

Hakuna mazungumzo au maneno ya kusemwa; sauti yao haisikiki

Misemo hii inaelza wazi kuwa mistari miwili ya kwanza ilikuwa sitiari. "Hakuna mazungumzo ya kweli wala maneo ya kusemwa; hakuna anyesikia sauti halisi kwa masikio yao"

sauti yao haisikiki

Tafsiri zingine zinasoma "ambapo sauti yao haisikiki," kusisitiza kuwa "mazungumzo" ya uumbaji yanapatikana kila sehemu.

Psalms 19:4

Taarifa ya Jumla:

Daudi amemaliza tu kusema kuwa uumbaji unaonesha utukufu wa Mungu.

maneno yao ...kusema kwao

Hii namaansiha "maneno" yasiyozungumzwa ya uumbaji yanayoonesha utukufu wa Mungu.

maneno yao huenda

Maneno yanaelezwa kana kwamba ni watu ambao wanatoka na ujumbe. "maneno amabyo uumbaji unazungumza ni kama watu wanaoenda nje"

kusema kwao hadi mwisho wa dunia

"kusema kwao kunaenda hadi mwisho wa dunia"

Ameweka hema kwa ajili ya jua

Hapa mwandishi anazungumzia sehemu ambayo Yahwe aliumba kwa ajili ya jua kana kwamba ni hema. "Aliumba sehemu kwa ajili ya jua"

miongoni mwao

Neno "mwao" inaweza kuwa inamaanisha mbingu.

Jua ni kama bwana arusi anayetoka katika chumba chake

Mwandishi anazungumzia kuchomoza kwa jua kana kwamba ni bwana arusi. "jua ni kama bwana arusi akitembea kwa furaha kwenda kwa bibi arusi wake"

kama mwamme menye nguvu anayefurahi anapokimbia mbio yake

Hii inalinganisha jua na mwanariadha kusisitiza nguvu na mwanga wa jua.

mwanamme mweye nguvu

"mkimbiaji mwenye kasi"

upeo wa macho

mstari ambao ardhi na anga hukutana

hadi mwingine

Hapa "mwingine" inamaanisha upeo wa macho. "hadi kwenye upeo wa macho mwingine"

hakuna kinachotoroka joto lake

Hii inaweza kuelezwa katika hali chanya. "kila kitu kinahisi joto lake"

Psalms 19:7

nafsi ... moyo ... macho

Maneno yote haya matatu yanamaanisha mtu mzima.

wa kawaida

"wale wasiokuwa na uzoefu" au "wale ambao hawajajifunza"

ni sahihi

"ni za kweli" au "ziko sawa"

huleta nuru

"huleta uelewa"

Psalms 19:9

pamoja ni sawa

"sahihi kabisa"

Zina thamani zaidi ya dhahabu ... nitamu zaidi ya asali

Amri za Yahwe zinazungumziwa kana kwamba zinaweza kununuliwa na kuonjwa. "Kama unaweza kuzinunua, zitakuwa na dhamani zaidi ya dhahabu ... kama unaweza kuzionja, zitakuwa tamu zaidi ya asali"

hata zaidi ya dhahabu safi

"hata thamani zaidi ya dhahabu nyingi safi"

dhahabu safi

"dhahabu halisi" au "dhahabu ya gharama"

Psalms 19:11

Ndio

"Pia" au "Kweli"

kwazo mtumishi wako huonywa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "zinamuonya mtumishi wako" au "ni onyo kwa mtumishi wako"

kwazo ...kwa kuzitii

Zinazozungumziwa hapa ni amri za Yahwe za haki.

mtumishi wako huonywa

Daudi anajiita "mtumishi wako" anapozungumza na Mungu kama ishara ya heshima. "nimeonywa"

Nani anaweza kutambua makosa yake yote?

Hii inaonekana katika hali ya swali kuongeza mkazo na inaweza kutafsiriwa na kauli kali. "Hakuna mtu anayeweza kutambua makosa yake mwenyewe!"

na makosa yaliyojificha

"na makosa ya siri niliyofanya"

Psalms 19:13

Muweke mtumishi wako pia mbali na

Lahaja hii inaonesha mtumishi kama ametolewa kwenye dhambi ambazo hataki kutenda. "Pia, mlinde mtumishi wako kutokufanya" au "Pia, hakikisha sifanya"

mtumishi wako

Daudi anajiita "mtumishi wako" anapozungumza na Mungu kama ishara ya heshima. "mimi"

usiziache zinitawale

Dhambi zinaelezwa kana kwamba ni mfalme anayeweza kutawala juu ya mtu. "usiache dhambi zangu ziwe kama mfalme anayetawala juu yangu"

sina hatia na makosa mengi

"sina hatia ya kuasi dhidi yako" au "sina hatia ya kutenda dhambi nyingi"

maneno ya mdomo wangu na mawazo ya moyo wangu

Misemo hii pamoja inaeleza kile ambacho mtu anasema na kuwaza. "vitu ninavyosema na vitu ninavyowaza"

yakubalike machoni pako

"yapokee kukubaliwa machoni pako" au "yakupendeze wewe"

machoni pako

Hii inamaanisha Mungu mwenyewe. "kwako"

Yahwe, mwamba wangu

Mwandishi anamzungumzia Mungu kana kwamba ni mwamba ambao mtu anaweza kupanda kujilinda dhidi ya adui zake. "Yahwe, wewe ni kama mwamba wangu"

Psalms 20

Psalms 20:1

Taarifa ya Jumla:

Zaburi hii inaanza na kundi la watu wakizungumza na mfalme wa Israeli.

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

ukusaidie

Anayesaidiwa hapa ni mfalme.

siku ya shida

Hapa "siku" inamaanisha muda mrefu zaidi. "nyakati za shida"

jina la Mungu wa Yakobo

Hapa "jina" linamaanisha Mungu mwenyewe. "Mungu"

Mungu wa Yakobo

hii inamaanisha babu yao Yakobo, aliyemwabudu Yahwe.

tuma msaada kutoka sehemu takatifu

Mungu kuwasaidia kutoka sehemu yake takatifu inazungumziwa kana kwamba Mungu alikuwa anatuma msaada. "na Yahwe awasaidie kutoka sehemu yake takatifu"

sehemu takatifu ... Sayuni

Zote hizi zinamaansiha hekalu la Mungu Yerusalemu.

Psalms 20:3

Na atilie akilini

Msemo huu "atilie akilini" ni njia nyingine ya kusema "akumbuke." Haimaanishi kuwa Mungu alisahau. Inamaanisha kutafakari au kuwazia. "Na akumbuke"

Na atilie

Hapa anayezungumziwa ni Yahwe.

Sela

Hili linaweza kuwa neno la kimuziki linalowaongoza watu jinsi ya kuimba au kujecheza vyombo hapa. Tafsiri zingine huandika neno hili la Kiebrania, na zingine haziliweki.

Na awape

"Na awapatie"

hamu ya moyo wako

Hapa "moyo" unamaanisha mtu mzima. Nomino dhahania "hamu" inaweza kuelezwa kama kitenzi. "unachotamani" au "unachotaka"

kutimiza mipango yako yote

Nomino dhania ya "mipango" inaweza kuelezwa kama kitenzi. "na akusaidie kutimiza kila jambo ulilopanga kufanya"

Psalms 20:5

tutafurahi katika ushindi wako

Hapa watakaofurahi ni watu. Watufurahi katika ushindi wa mfalme.

katika jina la Mungu wetu

Hapa "jina" linamaanisha heshima na sifa. "kwa heshima ya Mungu" au "kwa sifa ya Mungu wetu"

tutanyanyua bendera

"tutanyanyua mabango"

akupe maombi yako yote

"kukupa kila kitu unachomuomba"

Sasa

Neno hili linatumika kuweka mapumziko katika zaburi. Inahama kutoka kwa watu kuzungumza hadi kwa mfalme kuzungumza.

Ninajua

Anayejua inawezekana ni mfalme katika kipengele hiki.

mtiwa mafuta wake ... atamjibu ... atamuokoa

Mfalme anajizumzia mwenyewe katika hali ya mtu wa tatu. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya mtu wa kwanza. "mimi, mtiwa mafuta wake ... nijibu .. niokoe"

kutoka mbingu yake takatifu

Mungu anaishi mbinguni pamoja na kwenye hekalu Yerusalemu.

kwa nguvu ya mkono wake wa kuume unaoweza kumwokoa

Mkono wa kuume wa Mungu unaashiria nguvu yake kumwokoa mfalme. "kwa nguvu yake kubwa atamwokoa"

Psalms 20:7

Wengine wanatumaini vibandawazi na wengine farasi

Hapa "vibandawazi" na "farasi" zinamaanisha jeshi la mfalme.

na wengine farasi

Neno "tumaini" linaeleweka. "na wengine wantumaini farasi"

tunaita

Wanaoita ni mfalme na watu wake.

Wataletwa chini na kuanguka

Wanaoletwa chini ni watu wanaotumaini vibandawazi na farasi. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Mungu atawaleta chini na kuwafanya waanguke"

kuletwa chini na kuanguka

Vitenzi hivi viwili vinamana sawa. Zote mbili zinamaanisha kushindwa kwenye mapambano.

tutanyanyuka na kusimama wima

"tutainuka na kusimama wima." Misemo hii miwli inamaana ya kufanana. Zote mbili zinamaanisha ushindi katika mapambano.

Psalms 20:9

Yahwe, muokoe mfalme

Tafsiri zinazowezekana ni 1) watu wanamwomba Mungu kumlinda mfalme au 2) mfalme anaendelea kujizungumzia katika hali ya mtu wa tatu.

mfalme; tusaidie tunapokuita

Tafsiri zingine zinaelewa Kiebrania tofauti. Zingine zinatafsiri kama watu kuzungumza na Yahwe mfalme wao. "Mfalme, tusaidie tunapokuita"

Psalms 21

Psalms 21:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

katika nguvu yako, Yahwe

Inadokezwa kuwa hii ni nguvu ambayo Yahwe amempa mfalme kuwashinda adui zake. "kwa sababu wewe, Yahwe, umempa nguvu ya kutosha kuwashinda adui zake"

Jinsi gani anafurahi

"Anafurahi sana"

katika wokovu unaoutoa

Inadokezwa kuwa Mungu amemwokoa mfalme kutoka kwa adui zake. Nomini dhahania ya "wokovu" inaweza kuelezwa kama kitenzi. "kwa sababu umemwokoa kutoka kwa adui zake"

hamu zake za moyo

"matamanio ya moyo wake." Hapa "moyo" unamaanisha mtu mzima. "hamu yake" au "alichokuwa anatamani"

hujazuia

"haujamkatalia." Hii inaweza kuelezwa katika hali chanya. "umempa"

maombi ya midomo yake

Hapa "midomo" inaashiria mtu mzima. "maombi yake" au "kile alichokuomba"

Sela

Hili linaweza kuwa neno la kimuziki linalowaongoza watu jinsi ya kuimba au kujecheza vyombo hapa. Tafsiri zingine huandika neno hili la Kiebrania, na zingine haziliweki.

Psalms 21:3

unamletea baraka nyingi

Nomino dhahania "baraka" inaweza kuelezwa kama kitenzi. "unambariki sana" au "unampa vitu vingi vizuri"

umeweka kichwani mwake taji la dhahabu safi

Kuweka taji juu ya kichwa cha mtu ni ishara ya kumfanya kuwa mfalme.

taji la dhahabu safi

Hapa "dhahabu safi" inaashiria heshima kubwa anayopewa mfalme.

Aliomba uhai; ukampa

Nomino dhahania ya "uhai" inaweza kuelezwa kama kitenzi. "Alikuomba kuwa umfanye aishi kwa muda mrefu, ukaifanya itokee"

siku ndefu milele na milele

Maana zinazowezekana ni 1) maisha marefu sana au 2) masiha ya milele au 3) uzao mrefu.

Psalms 21:5

Utukufu wake

"heshima ya mfalme" au "umaarufu wa mfalme"

umeweka kwake fahari na utukufu

Kusababisha mfalme kuwa na utajiri na nguvu inazungumziwa kama fahari na utukufu ni vitu vilivyowekwa kwake. "umemfanya kuwa na utajiri na nguvu"

umempa

"umemruhusu kuwa na" au "umekubali kumpa"

baraka za kudumu

"baraka itakayodumu" au "baraka itayobaki"

furaha ya uwepo wako

"furaha ya kuwa katika uwepo wako" au "furaha inayokuja kwa kuwa karibu na wewe"

Psalms 21:7

katika uaminifu wa agano la aliye juu

"kwa kuwa aliye juu ni mwaminifu kwa agano lake"

hatasogezwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "hakuna mtu atakaye msogeza kama mfalme"

Mkono wako utakamata

Hapa "mkono" unaashiria nguvu. "Nguvu yako itakamta" au "Utawakamata kwa nguvu"

Mkono wako ... unachukia

Maana zinazowezekana za anaye zungumziwa ni 1) mfalme au zinamaanisha ni 2) Mungu.

Mkono wako wa kuume utawakamata wale wanaokuchukia

Hii inamaanisha kitu sawa kama sehemu ya kwanza ya sentensi. Inawekamkazo kuwa Mungu atampa mfalme uwezo wa kuwazuia adui zake.

Psalms 21:9

Katika kipindi cha hasira yako

"Utakapotokea katika hasira yako"

hasira yako ... Utaangamiza

Maana zinazowezekana za anaye zungumziwa ni 1) Mungu au ni 2) mfalme.

utawachoma kama tanuu ya moto

Yahwe au mfalme kuwaangamiza adui inazungumziwa kana kwamba adui ni mbao na Yahwe au mfalme atawatupa katika tanuu.

Yahwe atawamaliza katika gadhabu yake, na moto utawateketeza

Vishazi vyote viwili vina maana sawa. Yahwe kuwaangamiza kabisa adui zake inazungumziwa kana kwamba gadhabu yake ni moto unaowaunguza kabisa adui zake.

kutoka duniani ... kutoka kwa wanadamu

Misemo hii miwili inamaanisha kitu kimoja. Inaweka mkazo kuwa hakuna adui yao hata mmoja atakayepona.

Psalms 21:11

walikusudi

"walipanga." Waliopanga ni adui wa Mungu na mfalme.

maovu dhidi yako

"kufanya vitu viovu"

wakatunga njama

"wakafanya mpango" au "wakiunda hila"

Kwa kuwa utawageuza; utachukua upinde wako mbele yao

Maana zinazowezekana za anaye zungumziwa ni 1) mfalme au ni 2) Mungu na zinamzungumzia kana kwamba alikuwa ni shujaa mwenye upinde na mishale.

utawageuza

Hii ni njia ya kusema kuwa Mungu na mfalme watawashinda adui zao vitani.

utachukua upinde wako mbele yao

Hii inaashiria kuwa anawapiga adui zake kwa mishale.

Psalms 21:13

Utukuzwe, Yahwe, katika nguvu yako

Maana zinazowezekana ni 1) "Yahwe, tuoneshe kuwa una nguvu sana" (UDB) au 2) "Yahwe, kwa sababu una nguvu, tutakutukuza"

tutaimba na kusifu uwezo wako

Maneno "tutaimba" na "kusifu" yana maana ya kukaribiana. Hapa neno "uwezo" linamaanisha Mungu na uwezo wake. "kwa kuimba tutakusifu kwa sababu una uwezo"

Psalms 22

Psalms 22:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Mapigo ya mbawala

Hii inaweza kumaanisha aina ya muziki.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Mungu wangu, Mungu wangu

Mwandishi anarudia "Mungu wangu" kusisitiza kuwa anatamani sana Mungu amsikie.

Mungu wangu, kwa nini umeniacha?

Mwandishi anatumia swali kusisitiza kuwa anahisi kama vile Mungu amemwacha. Ni bora zaidi kuiacha hii kama swali. Inaweza pia kuwekwa kama kauli. "Mungu wangu, nahisi kama umeniacha!"

umeniacha

"umeniacha peke yangu"

Kwa nini uko mbali sana na kuniokoa na mbali na maneno yangu ya uchungu?

Mwandishi anatumia tena swali kusisitiza kuwa anahisi kama vile Mungu yuko mbali naye. Ni bora zaidi kuiacha hii kama swali. Inaweza pia kuwekwa kama kauli. "Uko mbali na kuniokoa na mbali na maneno ya uchungu wangu!"

mbali na maneno yangu ya uchungu

Mwandishi kuhisi kana kwamba Mungu hamsikilizi kunazungumziwa kana kwamba Mungu yuko mbali na maneno ya uchungu wake. Hapa "maneno" yanamaanisha chochote ambacho mwandishi anasema. "kwa nini hausikilizi ninapozungumza kwako kuhusu uchungu ninaoupitia" au "nimekuambia kuhusu mahangaiko yangu lakini haujaja kwangu"

mchana ... usiku

Mwandishi anatumia maneno "mchana" na "usiku" kumaanisha kuwa humwomba Mungu kila wakati.

siko kimya

Hii inaweza kuwekwa katika hali chanya. "Bado ninazungumza"

Psalms 22:3

umeketi kama mfalme na sifa za Israeli

"sifa za Israeli ni kiti cha enzi ambacho unaketi kama mfalme." Sifa za Israeli zinaelezwa kana kwamba ni kiti cha enzi ambacho Mungu anaketi na kutawala, au nyumba ambayo Mungu anaweza kuishi. "wewe ni mfalme na watu wa ISraeli wanakusifu"

za Israeli

Hapa "Israeli" inamaanisha watu wa Israeli.

hawakuvunjwa matarajio

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "na haukuvunja matarajio yao" au "haukuwaangusha"

hawakuvunjwa matarajio

Hii inaweza kuelezwa katika hali chanya. "na ukawaokoa" au "ukawafanyia walichohitaji uwafanyie"

Psalms 22:6

mimi ni mnyoo na sio mtu

Mwandishi anajizungumzia kana kwamba alikuwa ni mnyoo. Hii inaonesha mkazo kuwa alijihisi hafai au kuwa watu walimtenda kana kwamba hana faida. "Lakini ni kama mimi ni mnyoo na sio binadamu"

aibu kwa wanadamu na kuchukiwa na watu

Misemo hii miwili inamaana sawa. Msemo "kuchukiwa na watu" unaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "kila mtu anadhani sina faida na watu wananichukia"

wananidhihaki, wananifanyia mzaha; wanatikisa vichwa vyao kwangu

Misemo hii mitatu ina maana ya kukaribiana na inasisitiza jinsi watu walivyomdharau.

wanatikisa vichwa vyao kwangu

Hii inaelezea tendo ambalo watuwalitumia kumdhihaki mtu.

Anamtumaini Yahwe ... anamfurahia

Watu wanasema hivi kumdhihaki mwandishi. Hawaamani kweli kuwa Yahwe atamwokoa.

Acha amwokoe

"Acha Yahwe amwokoe"

kwa kuwa anamfurahia

Maana zinazowezekana ni 1) "kwa kuwa Yahwe anamfurahia" au 2) "kwa kuwa anamfurahia Yahwe"

Psalms 22:9

Kwa kuwa

Mwandishi anatumia neno "Kwa" kuanza kueleza kwa nini amechanganyikiwa na kumwuliza Mungu kwa nini haji kumsaidia.

umenitoa kwenye tumbo

Hii ni njia ya kusema "umesababisha nizaliwe"

nilipokuwa katika kifua cha mama yangu

Hii inamaanisha kuwa amekuwa akimtumaini Yahwe tangu yuko mchanga. "hata tangu wakati nilipokunywa maziwa kutoka kifua cha mama yangu"

Nimetupwa kwako kutoka tumboni

Msemo "nimetupwa" ni njia ya kusema kuwa Yahwe amemtunza kana kwamba Yahwe alimpanga utoto kama mwana wake. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Ilikuwa kana kwamba umenipanga utoto tangu nilipozaliwa"

wewe ni Mungu wangu

Hii inadokeza kuwa Yahwe daima amekuwa akimctunza mwandishi. "wewe, Mungu, umenitunza"

tangu nimo tumboni mwa mama yangu

"tangu kabla sijazaliwa"

Psalms 22:11

Usiwe mbali na mimi

Hii inaweza kuelezwa katika hali chanya. "Njoo karibu yangu"

kwa kuwa taabu iko karibu

Mwandishi anazungumzia "taabu" kana kwamba ni kitu kilicho karibu yake. "kwa kuwa adui zangu wako karibu yangu"

hakuna msaada

"hakuna msaidizi"

Mafahali wengi wamenizunguka; mafali hodari wa Bashani wamenizunguka

Mwandishi anawazungmzia adui zake kana kwamba ni mafahali. Hii inaweka mkazo wa jinsi adui zake walivyo na nguvu. "Nina adui wengi na wako kama mafahali wanaonizunguka; wako kama mafahali hodari kutoka Bashani wanaonizunguka"

Wamefungua midomo yao wazi dhidi yangu

Mwandishi anawazungumzia adui zake kana kwamba ni simba wenye midomo wazi tayari kumla. Adui zake wanaweza kuwa wanazungumza uongo kumpunguzia sifa. Au wanaweza kuwa wanamtisha na kumvamia.

kamasimba anayeunguruma akimrarua mhanga wake

Mwandishi anawazungumzia adui zake kana kwamba ni simba. Hii inasisitiza jinsi adui wake walivyokuwa na nguvu na hatari.

Psalms 22:14

Ninamwagwa nje kama maji

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Ni kama mtu ananimwaga nje kama maji"

Ninamwagwa nje kama maji

Mwandishi anazungumzia kuhusu kujihisi kuchoka na munyonge kana kwamba alikuwa maji akimwagwa nje ya chupa

mifupa yangu yote imeteguka

"mifupa yangu yote iko nje ya sehemu zake." Inawezekana mwandishi yuko katika aina flani ya maumivu ya kimwili. Au anaweza kuwa anazungumzia maumivu ya hisia kana kwamba ni maumivu ya kimwili.

Moyo wangu ni kama nta ... sehemu zangu za ndani

Mwandishi anazungumzia kutokuwa na ujasiri kana kwamba moyo wake umeyeyuka kama nta. Hapa "moyo" unaashiria "ujasiri."

nta

kitu laini kinacho yeyuka kwa joto dogo.

ndani ya sehemu zangu za ndani

"ndani yangu"

Nguvu yangu imekauka kama kipande cha ufinyanzi

Mwandishi anazungumzia kujisikia mdhaifu kana kwamba nguvu yake ilikuwa kama kipande cha ufinyanzi kilichokauka na chepesi kuvunjika.

kipande cha ufinyanzi

kitu kilichoundwa kwa udongo wa kuoka kinachoweza kutumika ndani ya nyumba.

ulimi wangu unatokeza hadi kwenye paa ya mdomo wangu

"ulimi wangu unatokeza hadi juu ya mdomo wangu." Mwandishi anaweza kuwa anaelezea kiu yake kali. Au anaweza kuwa anaendelea kuzungumzia kuwa mdhaifu kana kwamba amekauka kabisa.

Umenilaza kwenye vumbi la mauti

Maana zinazowezekana kwa ajili ya "vumbi la mauti" ni 1) inamaanisha mtu kugeuka kuwa vumbi baada ya kufa. "Unataka kuniacha nife na niwe vumbi" au 2) ni njia ya kuzungumzia kaburi, ambayo inamaanisha Mungu anamsababisha mwandishi kufa. "Umenilaza kwenye kaburi langu"

Umenilaza

Aliyemlaza ni Mungu.

Psalms 22:16

mbwa wamenizunguka

Mwandishi anazungumza kuhusu adui zake kana kwamba ni mbwa. Adui zake wanakuja karibu yake kama mbwa pori wanavyofanya kwa mnyama anayekufa. "adui zangu ni kama mbwa walionizunguka"

kundi la watenda maovu

"kikundi cha watenda maovu"

wamenizunguka

"wamenizingira"

wametoboa mikono yangu na miguu yangu

Hii inaendeleza mfano wambwa. Mwandishi anazungumzia adui zake kana kwamba ni mbwa wanao mng'ata na kutoboa mikono na miguu yake kwa meno yao.

toboa

kuchoma na kifaa chenye ncha kali

Ninaweza kuhesabu mifupa yangu yote

Maana zinazowezekana ni 1) mwandishi ni mwembamba sana hadi anaweza kuona mifupa yake. "Ninaweza kuona mifupa yangu yote" au "Ninaweza kuihisi mifupa yangu yote" au 2) hii inaendeleza mfano wa mbwa na mwandishi anaweza kuona mifupa yake baade ya mbwa kurarua nyama yake.

Wananitazama na kunikazia macho

Maneno "wananitazama" na "kunikazia macho" ina maana sawa na inasisitiza kuwa watu wanamwangalia kwa ajabu na kumtania.

Psalms 22:18

nguo zangu

"mavazi yangu"

Usiwe mbali

Hii inawezwa kuelezwa katika hali chanya. "Uwe karibu sana"

nguvu yangu

Hapa "nguvu" inaashiria Yahwe anayempa nguvu. "wewe unayenipa nguvu" au "wewe unayenisaidia"

Psalms 22:20

Okoa nafsi yangu

Hapa "nafsi" inamaanisha mtu mzima. "Niokoe"

upanga

Upanga ni njia ya kawaida ya kumaanisha adui mwenye vurugu. "wale wanaotaka kuniua" au "adui zangu"

maisha yangu pekee

"maisha yangu ya dhamani" au "maisha pekee niliyonayo"

makucha ya mbwa pori ... mdomo wa simba ... mapembe ya nyati

Mwandishi anawazungumzia adui zake kana kwamba ni mbwa, simba, na nyati kuweka mkazo jinsi adui zake walivyo hatari. Pia, makucha, mdomo, na mapembe yanamaanisha myama mzima. Mwandishi anasisitiza sehemu hizi za wanayama kwa sababu ndio sehemu ambazo wanyama hao hutumia kuua mtu.

mbwa pori ... nyati

Neno "pori" linamaanisha kuwa hakuna mtu aliyemshika na kumfuga huyu mnyama.

Psalms 22:22

Nitatangaza jina lako

"Nitafanya jina lako lijulikane." Hapa "jina" linaashiria tabia na sifa ya Mungu. "Nitazungumza kuhusu tabia yako"

ndugu zangu

Hapa "ndugu" inamaanisha "Waisraeli wezangu" au "waabudu wezangu wa Yahwe"

katikati ya kusanyiko

"Waisraeli wezangu na mimi tukikutana pamoja" au " ninapozungukwa na waabudu wezangu wa Yahwe"

Nyie mnayemwogopa

Hapa anazungumza na watu wengi.

Nyie wote uzao wa Yakobo ...nyie wote uzao wa Israeli

Zote hizi zinamaansiha kundi moja la watu.

Simameni kwa kumshangaa

"Mjawe na kumshangaa yeye" au "Acheni nguvu ya Mungu iwashangaze"

Psalms 22:24

hajadharau wala kuchukizwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali chanya. "amependa na kuona bora kabisa"

hajadharau wala kuchukizwa na mateso ya aliyeteswa

Hapa "mateso" inamaanisha mtu anayeteseka. "hajamdharau wala kumchukia yule anayeteseka"

hajadharau wala kuchukizwa

Maneno haya mawili yana maana ya kufanana na yanasisitiza kuwa Mungu hajamsahau mwandishi.

hajadharau

"chukia sana"

kuchukizwa

"kukemea"

mateso ya aliyeteswa ...kwake ... aliyeteswa alipolia

Hii inaweza kuelezwa ili imaanishe yeyote anayeteseka. "wale wanaoteseka ... kwao ... wale wanaoteseka walilia"

hajaficha uso wake

Hii ni lahaja. "hajageuza usikivu wake" au "hajaacha kunizingatia"

alisikia

"alisikiliza." Inadokezwa kuwa alijibu aliposikia kilio chao. "alijibu" au "alisaidia"

kwa sababu yako

Anayezungumziwa hapa ni Yahwe.

nitatimiza viapo vyangu

Hii inamaanisha sadaka ambazo mwandishi aliahidi kumtolea Mungu.

mbele yao

Ambaye wanamcha ni Yahwe. Inaweza kuelezwa kama "wewe." "mbele yao wanaokugopa wewe"

Psalms 22:26

Walidhulumiwa watakula na kuridhika

Hii inamaanisha mlo wa ushirika unaotokea baada ya mwandishi kumpa Mungu sadaka alizoahidi. Atawakaribisha wale waliokuwa wanateseka kula sehemu ya mnyama aliyemtoa sadaka.

wale wanaomtafuta Yahwe

Wale wanaotaka kumjua Yahwe na kumpendeza wanazungumziwa kana kwamba wanamtafuta Yahwe kwa uhalisia.

Mioyo yenu iishi milele

Hapa "mioyo" inawakilisha mtu mzima. "Na uishi milele"

Mioyo yenu

Hapa "yenu" inamaanisha watu walio dhulumiwa.

watakumbuka na kumgeukia Yahwe

Kuanza kumtii Yahwe kunazungumziwa kana kwamba watu wanamgeukia Yahwe kimwili. "watamkumbuka Yahwe na kumtii"

familia zote za mataifa zitasujudu chini mbele yako

Hii inamaanisha kitu kimoja na sehemu ya kwanza ya sentensi. Mwandishi anasisitiza kuwa kila mtu kutoka kila sehemu atamwabudu na kumtii Yahwe.

zitasujudu chini mbele yako

Hii ni alama ya kumpa utkufu na heshima mtu.

mbele yako

Hapa "yako" inamaanisha Yahwe. Inaweza kutafsiriwa katika hali ya mtu wa tatu ili ilingane na sehemu ya kwanza ya sentensi. "mbele yake"

Psalms 22:28

Kwa kuwa ufalme ni wa Yahwe

Hapa "ufalme" unaashiria utawala wa Mungu kama mfalme. "Kwa kuwa Yahwe ni mfalme"

yeye ni mtawala juu ya mataifa

Hapa "mataifa" yanaashiria watu wa mataifa. "anawatawala watu wa mataifa"

wata kuwa na karamu

Watu watakula pamoja kwenye karamu. "watakula pamoja" au "watakula chakula cha sherehe pamoja"

wale wote wanaoenda chini kwenye vumbi ... wale ambao hawawezi kuhifadhi maisha yao wenyewe

Misemo hii miwili inaashiria kundi moja. Zote zinamaanisha watu wote kwa kuwa watu wote watakufa.

wale wote wanaoshuka kwenye vumbi

Hapa "vumbi" linamaanisha kaburi. Msemo "wanaoshuka kwenye vumbi" ni njia ya kusema mtu anakufa. "wale wanaokufa" au "wale waliokufa"

wale ambao hawawezi kuhifadhi maisha yao wenyewe

"wale ambao hawawezi kuokoa maisha yao" au "wale ambao hawawezi kujizuia kufa"

Psalms 22:30

Kikazi kitakajokuja

Hapa "kizazi" kinawakilisha watu wa kizazi. "Msemo "kitakajokuja" inazungumzia muda wa baadaye kanakwamba ni kitu kinachosafiri na kufika sehemu. "watu wa vizazi vya baadaye"

kizazi kijacho

Hapa "kizazi" kinaashiria watu wa kizazi hicho. "watu wa kizazi kijacho" au "watoto wao"

cha Bwana

"kumhusu Bwana" au "kuhusu kile Bwana amefanya"

kusema kuhusu haki yake

Nomino dhahania ya "haki" inaweza kuelezwa kama kivumishi. "kusema kuhusu vitu vya haku alivyofanya"

Psalms 23

Psalms 23:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Yahwe ni mchungaji wangu

Mwandishi anamzungumzia Yahwe kana kwamba alikuwa mchungaji. Hii inasisitiza jinsi Mungu anavyowajali watu kama mchungaji anavyowajali kondoo wake. "Yahwe ni kama mchungaji kwangu" au " Yahwe ananijali kama mchungaji anavyojali kondoo wake"

sitapungukiwa kitu

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Nina kila kitu ninachohitaji"

Ananifanya kulala chini kwenye malisho ya kijani

Mwandishi anajizungumzia kana kwamba ni kondoo, na anamzungumzia Yahwe kana kwamba ni mchungaji. "Ananipa mapumziko kama mchungaji anavyowaongoza kondoo wake kulala chini kwenye malisho ya kijani"

ananiongoza kando kando na maji yaliyotulia

Mwandishi anajizungumzia kana kwamba ni kondoo, na anamzungumzia Yahwe kana kwamba ni mchungaji. "ananipa ninachohitaji kama mchungaji anayewaongoza kondoo wake kando kando ya maji matulivu"

maji yaliyotulia

"maji yanayotiririka taratibu." Maji haya ni salama kunywa.

Psalms 23:3

Taarifa ya Jumla:

Zaburi hii inaendelea kueleza jinsi Mungu anavyotujali kama kondoo anavyowajali kondoo wake.

Hurudisha maisha yangu

Hii inamaanisha Mungu anamfanya mtu aliyenyonge na mchovu kuwa na nguvu na kupumzika tena.

huniongoza katika njia zilizonyooka

Kumwonyesha mtu jinsi ya kuishi katika njia inayo mpendeza Mungu inazungumziwa kana kwamba ni mchungaji anaonesha kondoo njia sahihi ya kuchukua. "Ananionesha jinsi ya kuishi sawa"

kwa ajili ya jina lake

Msemo "jina lake" hapa unamaanisha sifa yake. "kwa ajili ya jina lake" au "ili watu wamheshimu"

Psalms 23:4

Taarifa ya Jumla:

Zaburi hii inaendelea kueleza jinsi Mungu anavyotujali kama mchungaji anavyojali kondoo wake.

Ingawa ninatembea katika bonde la kivuli cha giza zaidi

Mwandishi anamwelezea mtu anayepitia matatizo makubwa kana kwamba ni kondoo anayetembea kwenye bonde hatari la giza. Huko kondoo anaweza kupotea au kuvamiwa na mnyama pori. "Ingawa maisha yangu ni kama kutembea katika bonde hatari la giza"

sitaogopa madhara

Nomino dhahania ya "madhara" inaweza kuelezwa kama kitenzi. "Sitaogopa kitu kunidhuru"

uko nami

Aliye pamoja naye ni Yahwe.

gongo lako na fimbo yako hunifariji

Gongo na fimbo inaashiria ulinzi kwa sababu wachungaji walizitumia kuwalinda kondoo wao kutoka hatarini. "Siogopi kwa sababu unanilinda kama mchungaji anavyolinda kondoo wake kwa gongo na fimbo"

Psalms 23:5

Taarifa ya Jumla:

Sasa mwandishi anaeleza jinsi Mungu ni kama mtu anayemkaribisha mgeni nyumbani kwake na kumlinda.

Unaandaa

Meza inaashiria karamu kwa sababu watu huweka chakula chote mezani.

mbele ya adui zangu

Maana hapa ni kwamba mwandishi hana wasiwasi kuhusu adui zake kwa sababu yeye ni mgeni wa heshima wa Bwana na kwa hiyo analindwa na madhara. "licha ya uwepo wa adui zangu"

unatia kichwa changu mafuta

Watu wakati mwingine huweka mafuta kwenye vichwa vya wageni wao ili kuwapa heshima.

kikombe changu kinamwagikia

Hapa kikombe cha divai kinachotiririka kinaashiria baraka nyingi. "Unajaza kikombe changu sana hadi kinamwagikia" au "unanipa baraka nyingi"

Psalms 23:6

Hakika wema na uaminifu wa agano utanifuata

Yahwe kuwa mwema na mwaminifu kwa mtu inazungumziwa kana kwamba wema na uaminifu wa agano ni vitu vinavyomfuata mtu. "Hakika utakuwa mwema na mwaminifu kwangu"

siku zote za maisha yangu

Nomino dhahania ya "maisha" inaweza kutafsiriwa kama kitenzi. "maadamu nina ishi"

nyumba ya Yahwe

Maana zinazowezekana ni kwamba 1) hii inamaanisha nyumba ya milele ya Yahwe, au 2) hii inamaanisha hekalu la Yahwe Yerusalemu.

kwa muda mrefu sana

Maana zinazowezekana ni 1) "milele" au 2) "maadamu nina ishi."

Psalms 24

Psalms 24:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

na ujao wake

Nomino dhahania "ujao" inaweza kuelezwa kama kitenzi "kujaza." "na kila kitu kinachoijaza"

Kwa kuwa ameiweka juu ya bahari na kuiweka juu ya mito

Wahebrania wa wakati huo waliamini kuwa nchi ilishikiliwa na bahari na mito ya chini ya ardhi. "Kwa kuwa aliumba misingi yake kwenye bahari na kuijenga juu ya maji mrefu"

bahari ... mito

Misemo hii miwili inatumika kumaanisha bahari kubwa yenye kina kirefu chini ya dunia.

juu ya mito

"maji yaliyo chini kwenye kina kirefu"

Psalms 24:3

Nani ataupanda mlima ... katika sehemu yake takatifu?

Maswali yote haya mawili ya maana moja. Mwandishi anauliza kuhusu nani anayefaa kwenda kumwabudu Yahwe.

kupanda

"kwenda juu"

mlima wa Yahwe

Hii inamaanisha mlima Sayuni ndani ya Yerusalemu

sehemu yake takatifu

Hii inamaanisha hekalu la Yahwe. Hekalu lake liko katika mlima Sayuni ulioko Yerusalemu.

Yeye aliye ...aliye ... na haja...

Hapa haimzungumzii mtu bayana. "Wale ambao ...walio ... na hawaja..."

aliye na mikono safi

Neno "mikono" inawakilisha kile ambacho mtu anafanya. Kwa "mikono" kuwa safi inamaanisha anafanya kilicho sawa. "anafanya kilicho sawa"

moyo safi

Hapa "moyo" inamaanisha mawazo au nia ya mtu. "anawaza mawazo mazuri" au "hawazi kuhusu yaliyo mabaya"

ambaye hajainua juu uongo

Hapa "uongo" inawakilisha sanamu ya uongo. "Kuinua juu" inamaanisha kuabudu. "ambaye hajaabudu sanamu"

Psalms 24:5

Atapokea baraka kutoka kwa Yahwe

Hapa hazungumziwi mtu yeyote bayana. Inamaanisha wale wenye mioyo safi waliotajwa kwenye mstari uliopita. Nomino dhahania ya "baraka" inaweza kuelezwa kama kitenzi. "Yahwe atawabariki"

na haki kutoka kwa Mungu wa wokovu wake

Nomino dhahania ya "haki" inaweza kuelezwa kama "kwa haki." Na "wokovu" unaweza kuelezwa kama "okoa." "na Mungu atatenda kwa haki naye na kumwokoa"

Ndivyo kilivyo kizazi cha wale wanaomtafuta

Hapa "kizazi" inawakilisha watu kwa ujumla. "Watu wanaomtafuta wako hivi"

wale wanaomtafuta, wale wanautafuta uso wa Mungu wa Yakobo

Misemo yote miwili ina maana moja. Yote inamaanisha wale wanaoenda hekaluni kumwabudu Mungu. "wale wanaomkaribia Mungu, wao ndio wanaweza kumwabudu Mungu, yule ambaye sisi Waisraeli tunamwabudu"

wale wanaomtafuta

Kwenda hekaluni kumwabudu Yahwe inazungumziwa kana kwamba mtu anatafuta kwa uhalisia kumpata.

uso wa Mungu wa Yakobo

Hapa "uso" unamaanisha mtu mzima. "Mungu wa Yakobo"

Psalms 24:7

Inueni vichwa vyenu, nyie malango; muinuliwe, malango ya milele

Misemo miwili ina maana za kukaribiana. "Malango" ni ile ya hekaluni. Mwandishi anazungumza na malango kana kwamba ni mtu. Mtu anayetunza malango ndiye huwepo kufungua malango. "Fungukeni, enyi malango ya zamani" au "Fungueni milango hii ya zamani"

Inueni vichwa vyenu

Haikowazi ni sehemu gani bayana ya lango ndio "kichwa." Lakini inawakilishi mlango mzima kwa ujumla.

Yahwe, mwenye nguvu na hodari; Yahwe, hodari vitani

Mwandishi anamzungumzia Yahwe kana kwamba ni shujaa hodari anapigana vitani.

Psalms 24:9

Inueni vichwa vyenu, nyie malango; muinuliwe, malango ya milele

Misemo miwili ina maana za kukaribiana. "Malango" ni ile ya hekaluni. Mwandishi anazungumza na milango kana kwamba ni mtu. Mtu anayetunza malango ndiye huwepo kufungua malango. "Fungukeni, enyi malango ya zamani" au "Fungueni malango haya ya zamani"

Inueni vichwa vyenu

Haikowazi ni sehemu gani bayana ya lango ndio "kichwa." Lakini inawakilishi lango lote kwa ujumla.

Sela

Hili linaweza kuwa neno la kimuziki linalowaongoza watu jinsi ya kuimba au kujecheza vyombo hapa. Tafsiri zingine huandika neno hili la Kiebrania, na zingine haziliweki.

Psalms 25

Psalms 25:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

nainua maisha yangu

Msemo "nainua maisha yangu" ni sitiari. Maana zinazowezekana ni 1) mwandishi unajitoa kwa Yahwe, ambayo inamaanisha anamtegemea Yahwe kabisa. "nitajitoa kwako" au 2) aleta maombi na heshima kwa Yahwe. "ninakuabudu na kukuheshimu"

Usiniache niaibike

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Usiwaache adui zangu waniaibishe"

niaibike

"kudhalilika"

wafurahi kwa ushindi juu yangu

Msemo "juu yangu" unadokeza kuwa adui zake wamemshinda na kusima juu kwa ushindi. "wanishinde na kufurahia"

Na mtu yeyote anayekutumaini asiaibike

"Usiwaache wale wanaokutumaini waaibike." Aibu inaweza kuja kwa kushindwa na dui zao. Hii inaweza kuelezwa katika hali chanya. "Usiwaache adui wawashinde wale wanaokutumaini"

anayekutumaini

"wanaokuamini"

fanya udanganyifu

"fanya uongo" au "fanya ujanja"

bila sababu

"bila chanzo"

Psalms 25:4

Unijulishe njia zako, Yahwe; nifundishe njia zako

Kauli hizi mbili zina maana moja. Mungu kumfundisha mtu jinsi anavyotakiwa kutenda inazungumziwa kana kwamba alikuwa akimwonyesha mtu njia sahihi ambayo mtu anapaswa kusafiria.

Nakutumaini

"Nakutegemea" au "Nakusubiri kwa uvumilivu"

Niongoze kwenye kweli yako na unifundishe

Niongoze na unifundishe zina maana sawa, kutoa maagizo. "Nielekeze kusimamia maisha yangu kwa kutii ukweli wako"

Mungu wa wokovu wangu

Nomino dhahania ya "wokovu" inaweza kuelezwa kama "'huokoa." "yule anayeniokoa"

Psalms 25:6

Kuweka

Hii ni lahaja. Hii haimaanishi kuwa Mungu amesahau kitu. Mwandishi anamuomba kufikiria na kuzingatia matendo yake ya huruma na uaminifu. "Kumbuka" au "Fikiria kuhusu"

matendo yako ya huruma na uaminifu wako wa agano

Nomino dhahania za "huruma" na "uaminifu" zinaweza kuelezwa kama vivumishi. "jinsi ulivyokuwa na huruma na mwaminifu kwangu kwa sababu ya agano lako"

kwa kuwa wamekuwepo daima

Hapa zinazozungumziwa ni huruma na uaminifu wa Mungu. "kwa kuwa hivyo ndivyo ulivyokuwa daima"

Usiwaze kuhusu dhambi za ujana wangu

Nomino dhahania ya "dhambi" inaweza kuelezwa kama "kutenda dhami." "Usiwaze jinsi nilivyotenda dhambi dhidi yako nilipokuwa mdogo"

au ukaidi wangu

Nomino dhahania ya "ukaidi" unaweza kuelezwa kama "kukaida." "au kusuhu jinsi nilivyokaidi dhidi yako"

Weka akilini

Hii ni lahaja. Hii haimaanishi kuwa Mungu amesahau kitu. Hii haimaanishi kuwa Mungu alisahau kitu. Mwandishi anamwomba Mungu kumwaza. "Nikumbuke" au "Nifikirie"

na uaminifu wa agano kwa sababu ya wema wako

Nomino dhahnia za "uaminifu" na "wema" zinaweza kuelezwa kama vitenzi. "na uwe mwaminifu kwangu kwa sababu ya agano lako, kwa kuwa u mwema"

Psalms 25:8

njia ... njia yake

Jinsi amabvyo Mungu anataka mtu kuwa inazungumziwa kana kwamba ni njia ambayo mtu anasafiri.

wanyenyekevu

Hiki kivumishi kidogo kinaweza kuelezwa kama kivumishi. "watu wanyenyekevu" au "wale ambao ni wanyenyekevu"

Psalms 25:10

Njia zote za Yahwe ni upendo imara na uaminifu

"Yahwe hutupenda daima kwa sababu ya agano lake na ni mwaminifu daima"

Kwa ajili ya jina lako

Msemo "jina lako" hapa unamaanisha sifa ya Yahwe. "Kwa ajili ya sifa yako" au "Ili kwamba watu wakuheshimu"

samehe dhambi yangu, kwa kuwa ni kubwa

Nomino dhahania ya "dhambi" inaweza kuelezwa ka "kutenda dhambi." "tafadhali nisamehe, kwa kuwa nimetenda dhambi sana"

Psalms 25:12

Ni nani mtu anayemcha Yahwe?

Swali linatumbulisha "mtu anayemcha Yahwe" kama mada mpya. "Nitakuambia kuhusu mtu anayemcha Yahwe"

mtu anayemcha ... mwelekeza ... anapaswa ... Maisha yake ...uzao wake

Hii haimaanisha mtu bayana. "ni wale wanaomcha ... anawaelekeza ... wanapaswa ... Maisha yao ... uzao wao"

Bwana atamuelekeza katika njia anayopaswa kuchagua

Yahwe kuwafundisha watu jinsi wanavyopaswa kuwa inazungumziwa kana kwamba Yahwe alikuwa akiwafundisha watu ni njia gani wanapaswa kuifuata.

Maisha yake yataenda katika wema

"Mungu atamsababisha kufanikiwa" au "Mungu atawasababisha kufanikiwa"

Psalms 25:14

Urafiki wa Yahwe ni kwa wale

"Yahwe ni rafiki kwa wale." Wengine wanatafsiri hii kama "Yahwe anawaambia siri wale." Kuwaambia siri inaonesha urafiki wa karibu alionao nao.

Macho yangu daima yako kwa Yahwe

Hapa "macho" yawakilisha kuangalia. kumwangalia Yahwe ni njia ya kusema anamuomba Yahwe msaada. "Huwa natazama kwa Yahwe" au "Huwa namuomba Yahwe msaada"

kwa kuwa ataokoa miguu yangu kwenye wavu

Wavu ni mtego. Mtu aliye hatarini anazungumziwa kana kwamba miguu yake imekwama katika wavu. "Ataniokoa katika

Geukia kwangu

Yahwe kuzingatia mtu kwa makini inazungumziwa kana kwamba Yahwe alikuwa akigeuka kimwili kuelekea kwa mtu huyo.

Psalms 25:17

Taabu za moyo wangu zimekuwa

Hapa "moyo" unawakilisha hisia za mtu. "Najihisi kutaabika zaidi na zaidi"

nitoe katika dhiki yangu

"nitoe kwenye dhiki yangu." Hii inazungumzia dhiki kana kwamba ni sehemu ambayo mtu anaweza kutolewa. "niokoe na dhiki yangu" au "nipumzishe na dhiki yangu"

dhiki zangu

Neno "dhiki" ni nomino dhahania. "vitu vinavyonipa dhiki" au "vitu vinavyosababisha niogope"

Tazama mateso yangu

"Tambua mateso yangu"

mateso yangu

Nomino dhahania ya "mateso" inaweza kuelezwa kama kitenzi. "vitu vinavyonitesa" au "jinsi nilivyoteseka"

taabu zangu

Neno "taabu" ni nomino dhahania. "vitu vinavyonipa taabu"

wananichukia na chuki ya kikatili

"wananichukia kwa ukatili" au "wananichukia kwa ukali"

Psalms 25:20

usiniache niaibike

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Usiwaache adui zangu waniaibishe"

ninakukimbilia wewe!

Kwenda kwa Yahwe kwa ajili ya ulinzi inazungumziwa kama kumkimbilia. "kwenda kwako kwa ajili ya ulinzi!"

Na uadilifu na unyofu unihifadhi

Hii inazungumzia "uadilifu" na "unyofu" kana kwamba ni watu wanaoweza kumweka mtu mwingine salama. Nomino dhahania hizi zinaweza kuelezwa kama vivumishi. "Na kuwa mwaminifu na kufanya kilicho sawa kilihifadhi" au "Nihifadhi, Bwana, kwa kuwa mimi ni mwaminifu na hufanya kilicho sawa"

unihifadhi

"uniweke salama"

Psalms 25:22

Iokoe Israeli

"Komboa Israeli"

Israeli ... shida zake

Hapa "Israeli" inawakilisha watu wa Israeli. "watu wa Israeli ... shida zetu"

Psalms 26

Psalms 26:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Nimetembea

Neno "kutembea" ni sitiari ya tabia. "Nimeenenda"

Yahwe

Matumizi ya mtu wa tatu wa "Yahwe" inaweza kuelezwa katika hali ya mtu wa pili. "wewe"

bila kuyumba

Mashaka yanazungumziwa kana kwamba ilikuwa ni kuyumba na kupepea mbele na nyuma. "bila kuwa na shaka"

Nichunguze

"Nijaribu"

jaribu usafi wa sehemu zangu za ndani na moyo wangu

Hapa "sehemu za ndani" na "moyo" inamaanisha nia. "jaribu kama nia zangu ni nzuri"

Kwa kuwa uaminifu wako wa agano uko mbele ya macho yangu

Hapa "macho" yanawakilisha mawazo ya mtu. "Kwa kuwa huwa nawaza kuhusu jinsi ulivyo mwaminifu kwangu kwa sababu ya agano lako"

ninatembea katika uaminifu wako

Neno "kutembea" ni sitiari ya tabia. "Ninaendesha maisha yangu kulingana na uaminifu wako" au "Ninaenenda jinsi nilivyo kwa sababu ya uaminifu wako"

Psalms 26:4

Sijihusishi

"Sikai kundi moja na" au "Siketi na"

na watu waongo

"na wale wanao wadanganya wengine"

wala kujichanganya na watu wasio wakweli

Hii ina maana sawa na sehemu ya kwanza ya sentensi. "na sijiungi na watu wasio wakweli"

watu wasio wakweli

"wanafiki" au "wale wanao wadanganya wengine"

mkusanyiko wa watenda maovu

"wale wanao kusanyika kutenda maovu"

waovu

Hiki ni kivumishi kidogo. "watu waovu" au "wale walio waovu"

Psalms 26:6

Ninanawa mikono yangu katika sehemu isiyo na hatia

Hii inaonekana kumaanisha utaratibu wa kunawa mikono kwatika maji kuashiria uhuru kutoka dhambini au hatia.

kuizunguka madhabahu yako

Hili lilikuwa tendo la kuabudu amablo Waisraeli walizoea kufanya.

nyumba unayoishi

Maana zinazowezekana ni 1) kama mtu aliandiki hii baada ya wakati wa Daudi, basi mwandishi anamaanisha hekalu liliko Yerusalemu. au 2) kama Daudi aliandiki hii, basi hii inamaanisha hema ambalo Mungu aliwaambia watu wake kuandaa ili wamwabudu humo.

sehemu ambayo utukufu wako huishi

Hapa "utukufu" unawakilisha uwepo na nguvu ya Mungu, ambayo inakaribiana na mwanga mweupe sana. "sehemu ambayo watu wanaweza kuona mwanga wako mtukufu wa uwepo wako"

Psalms 26:9

usinifagie na watenda dhambi

"kufagia" ni sitiari ya maangamizi. "Usiniangamize pamoja na watenda dhambi"

au maisha yangu

Neno "fagia" linaeleweka. "au usifagie maisha yangu"

watu wenye kiu ya damu

Maneno "kiu ya damu" yanawakilisha mtu anayetaka kuua watu wengine. "watu wenye hamu ya kumwaga damu ya wengine" au "watu wauaji"

ambamo minono yao

"Mikono" inashiria mtu mzima. "watu ambao"

njama

"mpango uovu"

Psalms 26:11

Lakini kwangu

Msemo huu unaonesha kuwa mwandishi anabadilisha kutoka kuwazungumzia watu waovu na kujizungumzia mwenyewe.

nitatembea kwa uadilifu

"Kutembea" ni sitiari ya tabia. "Nitaenenda kwa uadilifu"

Mguu wangu unasimama

Hapa "mguu" unawakilisha mtu mzima. "Nina simama"

ardhi tambarare

Maana zinazowezekana ni kwamba "ardhi tambarare" inawakilisha 1) sehemu salama au 2) tabia iliyo sawa

katika makusanyiko nitambariki Yahwe

"nitakapowakusanya watu wa Israeli nitakusifu"

Psalms 27

Psalms 27:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Yahwe ni nuru yangu

Hapa "nuru" inawakilisha maisha. "Yahwe ni chanzo cha maisha yangu"

nimwogope nani?

Swali hili linaweka mkazo kuwa hakuna mtu ambaye Daudi anapaswa kumwogopa. "sitamwogopa mtu yeyote"

Yahwe ni kimbilio langu

Hii inamzungumzia Yahwe kana kwamba ni sehemu ambapo watu wanaweza kwenda kwa ajili ya usalama. "Yahwe ndiye anayeniweka salama"

nimhofu nani?

Swali hili linaweka mkazo kuwa hakuna mtu ambaye Daudi anapaswa kumwogopa. "sitamhofua mtu yeyote"

Psalms 27:2

kuteketeza mwili yangu

Kumwangamiza mtu kabisa inazungumziwa kana kwamba ni kuangamiza mwili wa mtu. Hamaanishi kwamba walitaka kula mwili wake. "kuniangamiza"

washindani wangu na adui zangu

Maneno haya yana maana sawa. Hawa ndio watenda maovu walisogea karibu yake.

walijikwaa na kuanguka

Hii inaashiria adui wa mwandishi kushindwa kutimiza mipango yao kumdhuru mwandishi. "hawakufanikiwa"au "walishindwa"

Ingawa jeshi linweka kambi dhidi yangu

"ingawa jeshi linanizunguka" au "ingawa jeshi linanizunguka na mahema"

moyo wangu hautaogopa

Hapa "moyo" unawakilisha mtu mzima. "Sitaogopa"

ingawa vita zinainuka

Adui wa mwandishi wanazungumziwa kana kwamba wao wenyewe wako vitani. "ingawa adui zangu wanakuja kupigana na mimi"

nitabaki na ujasiri

"nitaendelea kumtumaini Mungu kunisaidia"

Psalms 27:4

nimemuomba Yahwe

"nimemuomba Yahwe kuniruhusu"

nitaitafuta hiyo

Mtu anayetaka kitu sana na kumwomba Mungu mara kwa mara kwa ajili yake inazungumziwa kama kutafuta kitu.

kuona uzuri wa Yahwe

Tabia nzuri ya Mungu inazungumziwa kana kwamba ni uzuri ya kimwili. "kuona jinsi Yahwe alivyo mzuri"

kutafakari katika hekalu lake

Maana zinazowezekana ni 1) "kumwuliza Mungu anataka nifanye nini" au 2) "kumtafakari Mungu kwa makini katika hekalu lake"

Psalms 27:5

katika siku ya taabu

Hapa "siku" inawakilisha muda mrefu zaidi. "katika wakati wa taabu" au "ninapokuwa na taabu"

atanificha

"atanilinda"

kivuli chake ... hema lake

Zote hizi zinamaanisha hema ambamo mwandishi anamwabudu Mungu.

katika mfuniko wa hema lake

Neno "mfuniko" inawakilisha kitu kinachoficha na kulinda.

Ataniinua juu ya mwamba

Mungu kumweka salama mwandishi kutoka kwa adui zake inazungumziwa kanakwamba Mungu alimuweka katika mwamba wa juu ambapo adui zake hawakuweza kumfikia.

kichwa changu kitainuliwa juu ya adui zangu

Hii inawakilisha mwandishi kupokea sifa au heshima anapowashinda adui zake. Inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "watu wataniheshimu nitakaposhinda pambano langu dhidi ya adui zangu" au "Mungu atanipa heshima kwa kuniwezesha kuwashinda adui zangu"

Psalms 27:7

Sikia, Yahwe, sauti yangu

Hapa "sauti" inamaanisha kuwa mwandishi anasema. "Nisikie, Yahwe"

nijibu

Hii inaashiria kuwa Yahwe anasikia maombi ya mwandishi na Yahwe atafanya kile mwandishi anachoomba. "jibu ombi langu" au "fanya ninachokuomba"

Moyo wangu unasema

Hapa "moyo" unawakilisha akili na mawazo ya mtu. "Moyoni mwangu nasema" au "Ninajiambia"

Utafute uso wake

Mtu kwenda hekaluni kumwomba Yahwe inazungumziwa kana kwamba mtu huyo anamtafuta Yahwe. "Hapa "uso" unamwakilisha Mungu. "Nenda ukaombe kwa Yahwe"

Nautafuta uso wako, Yahwe

Mtu kwenda hekaluni kumwomba Yahwe inazungumziwa kana kwamba mtu huyo anamtafuta Yahwe. "Hapa "uso" unamwakilisha Mungu. "Nitakuja kwenye hekalu lako na kuomba kwako"

Psalms 27:9

Usiufiche uso wako kwangu

Uso unawakilisha usikivu wa Yahwe. Msemo "Usiufiche uso wako" ni njia kumwomba Mungu asimkatae. "Usinikatae" au "Usiache kunitunza"

usimgeuza mtumishi wako kwa hasira

Daudi alisema "mtumishi wako" kumaanisha ni yeye mwenywe kwa njia ya unyenyekevu. "usinikasirikie"

usiniache wala kunitupa

Maneno "kuacha" na "kutupa" yana maana sawa. Mwandishi anasisitiza kuwa hataki Mungu amuache.

wala kunitupa

"na usinitupe" au "na usiniache"

Mungu wa wokovu wangu

Nomino dhahania ya "wokovu" inaweza kuelezwa kama "okoa." "Mungu anayeniokoa" au "kwa kuwa wewe ni Mungu unayeniokoa"

Hata kama baba na mama yangu wakiniacha

Hasemi kuwa kweli wamefanya hivi au kwamba watafanya hivi. Wazo lake ni kwamba hata kama wangefanya hivyo, Mungu asingemuacha.

Yahwe atanichukua

"Yahwe atanitunza"

Psalms 27:11

Nifundishe njia yako

Jinsi mtu anavyopaswa kuenenda inazungumziwa kana kwamba ni njia ambayo mtu anapaswa kusafiri. "Nifundishe jinsi unavyotaka niishi" au "Nifundishe unachotaka nifanya"

Niongoze katika njia tambarare

Yahwe kumweka mwandishi salama na adui zake inazungumziwa kana kwamba Yahwe anamwongoza mwandishi katika njia tambarare ambapo hatajikwaa na kuanguka. "Niweke salama"

Usiniweka katika hamu za adui zangu

Nomino dhahania ya "hamu" inaweza kuelezwa kama kitenzi. "Usiwaache adui zangu wafanye kwangu wanachotamani"

wameinuka dhidi yangu

"Kuinuka" ni lahaja inayomaanisha kuwa shahidi alisimama mahakamani kutoa ushuhuda. "wamesimama ili kuzungumza dhidi yangu"

wanapumua vurugu

Hapa vurugu inazungumziwa kana kwamba ilikuwa ni kitu ambacho mtu anaweza kupumua nje. "wanasema kwamba watafanya vitu vya vurugu kwangu"

Psalms 27:13

Nini kingetokea kwangu

Swali hili balagha linaweza kuelezwa katika hali chanya. "Kitu kibaya kingetokea kwangu"

uzuri wa Yahwe

Nomino dhahania ya "uzuri" inaweza kuelezwa kama kitenzi. "vitu vizuri ambavyo Yahwe hufanya"

katika nchi ya walio hai

Hii inamaanisha kuwa hai. "wakati niko hai"

Msubiri Yahwe ... msubiri Yahwe!

Mstari huu unaweza kuwa 1) mwandishi anazungumza mwenyewe au 2) mwandishi anazungumza na wengine au 3) mtu anazungumza na mwandishi.

acha moyo wako uwe na ujasiri

Hapa "moyo" unawakilisha mtu mzima. "uwe mjasiri"

Msubiri Yahwe!

Mstari huu umerudiwa mwishoni mwa zaburi kama njia ya kumalizia zaburi.

Psalms 28

Psalms 28:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

ninalia

"ninaita kwa sauti"

mwamba wangu

Hii ni sitiari ya nguvu. "nguvu yangu"

usiache kunijali

"usiwe kimya kwangu" au "usiniache mwenyewe"

Nitaungana na wale wanaoenda chini kaburini

Watu wanaokufa wanazungumziwa kana kwamba wanaenda kaburini. "Nitakufa kama wale waliomo kaburini"

Sikia sauti ya dua yangu

Hapa "sauti" inamaanisha maneno ya ombilake. "Sikia ombi langu kuu"

Napainulia mikono yangu mahali pako patakatifu

Kuinua mikono ni ishara ya kuabudu. Mwandishi haabudu mahali patakatifu, bali Yahwe anayeishi katika sehemu hiyo takatifu.

mahali pako patakatifu

Maana zinazowezekana ni 1) kama Daudi aliandika hii, basi hii inamaanisha hema ambalo Mungu aliwaambia watu wake kuandaa ili wamwabudu humo, au 2) kama ni mtu aliandika baada ya wakati wa Daudi, basi mwandishi anamaanisha hekalu lililoko Yerusalemu.

Psalms 28:3

Usinikokote

Mungu kuwaadhibu inazungumziwa kana kwamba anawakokota kimwili. Katika sitiari hii, Yahwe anaweza kuwa anawakokota kwenda gerezani, uhamishoni, au kifoni. "Usinitoe"

ambao wanazungumza amani na majirani zao

Hapa "majirani" inamaanisha watu kwa ujumla. "wanazungumza kwa amani na watu wengine"

lakini wana uovu mioyoni mwao

Hapa "mioyo" inawakilisha akili au mawazo ya mtu. "lakini wanawaza kitu kiovu kuwahusu"

Wape kile ambacho matendo yao maovu yanastahili ... walipe kile ambacho uovu wao unadai

Misemo hii miwili ina maana sawa. Inatumika pamoja kusisitiza kuwa wanastahili kuadhibiwa na Mungu.

kazi ya mikono yao

Hapa "mikono" inawakilisha kile ambacho mtu amaefanya"

warudishie wanachostahili

"wape wanachostahili"

Kwa sababu hawaelewi ... usiwajenge tena

Haiko wazi kama mstari wa 5 unaeleweka kama kauli au ombi.

hawaelewi matendo ya Yahwe

Inadokezwa kuwa "hawaelewi" inamaanisha hawajali au kuheshimu kazi za Yahwe. "hawajali kwa heshima kile ambacho Yahwe amefanya"

kazi ya mikono yake

Hapa "mikono" inawakilisha kile ambacho Yahwe amefanya au kuumba. "alichoumba"

atawavunja chini na hatawajengea tena

Adhabu ya watu waovu inazungumziwa kana kwamba walikuwa wakijenga mji utakaoangamizwa.

Psalms 28:6

amesikia sauti ya dua yangu

Hapa "sauti" inawakilisha kile mwandishi alichosema. "amesikia nilichosema nilipomwomba"

Yahwe ni nguvu yangu

"Yahwe ananifanya kuwa na nguvu"

ngao yangu

Hii inawakilisha ulinzi wa Yahwe kwa mwandishi.

moyo unamtumaini

Hapa "moyo" unamwakilisha mtu mzima. "Ninamwamini"

ninasaidiwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali yakutenda. "ananisaidia"

moyo unafurahi sana

Hapa "moyo" unamwakilisha mtu mzima. "ninafurahi sana"

Yahwe ni nguvu ya watu wake

"Yahwe anawafanya watu wake kuwa na nguvu"

ni kimbilio la wokovu la mtiwa mafuta wake

Yahwe kumweka mfalme salama inazungumziwa kana kwamba Yahwe ni sehemu ambayo mfalme anaweza kwenda kwa ajili ya usalama. "anamuweka salama yule aliyemchagua kuwa mfalme"

mtiwa mafuta wake

Hii inamaanisha mfalme.

Psalms 28:9

urithi wako

Hii inazungumzia watu wa Mungu kana kwamba walikuwa kitu ambacho Mungu alirithi. "mali yako" au "wale walio wako"

Uwe mchungaji wao na uwabebe milele

Mwandishi anazungumza kumhusu Yahwe kana kwamba ni mchungaji na watu ni kondoo wake. Mchungaji humbeba kondoo kama anahitaji msaada au ulinzi. "Uwe kama mchungaji na uwalinde milele"

Psalms 29

Psalms 29:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

wana wa Mungu

Msemo "wana wa" ni njia ya kusema "kuwa na sifa za." "nyie watu hodari"

Mpeni sifa kwa Yahwe kwa utukufu wake na nguvu

Nomino dhahania ya "utukufu" na "nguvu" zinaweza kuelezwa kama vitenzi. "Mpeni heshima Yahwe kwa kuwa ana utukufu na nguvu"

Mpeni Yahwe utukufu ambao jina lake linastahili

Nomino dhahania ya "heshima" inaweza kuelezwa kama kitenzi. "Mheshimu Yahwe kama ambavyo jina lake linastahili" au "Tangazeni kuwa Yahwe ni mtukufu kama jina lake linavyostahili"

ambao jina lake linastahili

Msemo "jina lake" unamaanisha Yahwe au sifa yake. "kama ilivyo sahihi kwa sababu alivyo"

Psalms 29:3

Taarifa ya Jumla:

Zaburi hii inaonesha nguvu na utukufu wa Yahwe.

Sauti ya Yahwe inasisikika juu ya maji

Sauti ya Mungu ni kubwa na inasikika vizuri zaidi ya sauti na kelele zingine. Inaweza kusikika juu ya sauti zingine kubwa kama sauti ya maji. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe akizungumza sauti yake ni kubwa zaidi ya sauti ya bahari" au "Yahwe anapaza sauti zaidi ya sauti ya maji"

juu ya maji

Hii inamaanisha bahari. Maji haya hutoa sauti kubwa sana mawimbi yanapopanda na kushuka.

Sauti ya Yahwe

"Sauti" katika sehemu zote hapa inamwakilisha Yahwe akizungumza. Mwandishi anasisitiza kuwa wakati Yahwe anazungumza, sauti ni kubwa sana inasikika juu ya maji, na ina nguvu sana inaweza kuangamiza miti mikubwa . "Yahwe akizungumza, sauti yake"

Mungu wa utukufu anapiga radi

Hii inazungumzia juu ya Mungu kuzungumza kana kwamba ilikuwa ni sauti ya radi. Kama tu sauti ya radi, sauti ya Yahwe inaweza kusikika umbali mrefu. "Sauti ya Mungu wa utukufu ni kama radi kubwa" au "Wakati Mungu wa utukufu akizungumza inaunguruma kama radi"

juu ya maji mengi

"juu ya maji mengi"

Psalms 29:6

Kauli Unganishi:

Mwandishi anaendelea kuelezea nguvu ya sauti ya Mungu.

Anaifanya Lebanoni kurukaruka kama ndama

Lebanoni inazungumziwa kana kwamba ni ndama mchanga. Hii inasisitiza kwamba Yahwe akizungumza, nguvu ya sauti yake hutikisa ardhi. "Hufanya nchi ya Lebanoni kutikisika kama ndama anaye rukaruka"

kurukaruka

kuruka kidogo hapa na pale

Sirioni kama kama ng'ombe mdogo

Sirioni inazungumziwa kana kwamba ni ng'ombe mchanga. Hii inasisitiza kuwa Yahwe akizungumza, nguvu ya sauti yake hutikisia ardhi. "Huifanya Sirioni kuruka kama ng'ombe mchanga"

Sirioni

Huu ni mlima Lebanoni. Pia unaitwa mlima Hermoni.

Sauti ya Yahwe inatuma miali ya moto

Sehemu zote zenye "sauti" zinamaanisha Yahwe anazungumza. "Yahwe akizungumza husababisha miali ya radi kuonekana angani"

miali ya moto

hii inamaanisha mwale wa radi.

Psalms 29:9

Sauti ya Yahwe husababisha

Hapa "sauti" inamaanisha Yahwe anazungumza. "Yahwe akizungumza, sauti husababisha"

mwaloni kujikunja

"miti mikubwa kutikisika"

na kuuvua msitu

Kutoa majani ya miti inazungumziwa kana kwamba ilikuwa kuvua nguo zao. "hutoa majani kwenye miti"

Yahwe ameketi kama mfalme

Hii inamaanisha kuwa Yahwe anatawala. "Yahwe anatawala" au "Yahwe ni mfalme"

juu ya mafuriko

Hapa "mafuriko" yanamaanisha maji yanayofunika dunia.

Psalms 29:11

Yahwe anawabariki watu wake na amani

Neno "amani" ni nomino dhahania. Yahwe huwabariki watu wake kwa kuwasababisha kufanikiwa na kuishi kwa amani"

Psalms 30

Psalms 30:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

wimbo wakati wa kuweka wakfu hekalu

"Huu wimbo uliimbwa wakati hekalu linawekewa wakfu"

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

umeniinua

Mwandishi anazungumzia Mungu kumwokoa na kumwepusha na kufa kana kwamba Mungu amemuinua kutoka katika kisima kirefu. "umeniokoa"

umeinua nafsi yangu kutoka kuzimu

Kwa kuwa "kuzima" ilikuwa sehemu ambapo wafu huenda, inamaanisha kifo. "umeniepusha na kifo"

umeinua nafsi yangu

Hapa "nafsi yangu" inamaanisha mwandishi. "umenileta juu"

na kwenda chini kaburini

"Kaburi" linawakilisha kifo. "na kufa"

Psalms 30:4

Mpeni shukrani mnapo kumbuka utakatifu wake

Nomino dhahani "utakatifu" inaweza kuelezwa kama "takatifu." "Kumbukeni kuwa Mungu ni mtakatifu na mshukuruni" au "Kumbukeni kile ambacho Mungu amefanya kwa kuwa ni mtakatifu na mshukuruni"

hasira yake ni kwa muda tu

"hasira ya huduma kwa muda tu." Nomino dhahania ya "hasira" inaweza kuelezwa kama "kasirika." Anakasirika kwa muda tu"

muda

Hapa "muda" inaashiria muda mdogo. "muda mfupi"

lakini fadhila zakeni milele

Nomino dhahania ya "fadhila" inaweza kuelezwa kama kivumishi "mwema." "lakini yeye ni mwema kwetu maisha yetu yote"

Kulia kunakuja usiku, lakini furaha huja asubuhi

Hii inazungumzia "kulia" na "furaha" kana kwamba ni vitu vinavyo safiri na kufika kwa wakati fulani. "Tunaweza kulia wakati wa usiku, lakini asubuhi ijayo tutakuwa na furaha"

Psalms 30:6

Kwa ujasiri

Neno "ujasiri" ni nomino dhahania. Mwandishi anakumbuka kipindi alipokuwa akifanikiwa na kujihisi kuwa na ujasiri na salama. "Nilipokuwa na ujasiri" au "Nilipojihisi kuwa salama"

Sitatikiswa kamwe

Neno "kutikiswa" ni sitiari ya kushindwa. "Hakuna atakayenishinda"

kwa fadhila zako

Nomino dhahania "fadhila" inaweza kuelezwa kama kitenzi "pendelea" au kivumishi "huruma". "uliponipendelea" au "ulipokuwa na huruma kwangu"

umeniweka kama mlima imara

Usalama wa mwandishi unazungumziwa kana kwamba alikuwa mlima imara. "umenifanya salama kama mlima ulio juu"

ulipoficha uso wako

Hii ni lahaja. "ulipoacha kunisaidia" au "uliponikataa"

nilipata taabu

"niliogopa" au "nilikuwa na wasi wasi"

nikatafuta fadhila kutoka kwa Bawana wangu

Msemo "nikatafuta fadhila" inamaanisha kuomba msaada. "nilikuomba unisaidie"

kutoka kwa Bawana wangu

Mwandishi anamaanisha Yahwe katika hali ya mtu wa tatu. Inaweza kuelezwa katika hali ya mtu wa pili. "kutoka kwako, Bwana wangu"

Psalms 30:9

Kuna faida gani ... kuwa msaidizi wangu

Hii inaweza kuelezwa kama nukuuya moja kwa moja.

Kuna faida gani katika kifo changu, kama nikienda kaburini?

Mwandishi anatumia swali hili kusisitiza kuwa hatakuwa wa faida kwa Mungu kama akifa. "Hakuna faida katika kufa kwangu na kwenda chini kaburini"

Je, mavumbi yatakusifu? Yatatangaza uaminifu wako?

Mwandishi anatumia maswali haya kusisitiza kuwa mwili wake uliokufa na kuoza hauwezi kumsifu Mungu. "Mavumbi yangu hakika hayatakusifu au kuwaambia watu jinsi ulivyo mwaminifu"

mavumbi

Hii inamaanisha mwili wa mwandishi utakaooza na kuwa mavumbi atakapokufa. "mwili wangu uliooza"

Psalms 30:11

Umegeuza kuomboleza kwangu kuwa kucheza

Ili kuwa ni utamaduni kwa Wayahudi kucheza walipokuwa na furaha. Nomino dhahania "kuomboleza" na "kucheza" zinaweza kuelezwa kama vitenzi. "Umenisababisha niache kuomboleza na badala yake kucheza kwa furaha"

umeliondoa gunia langu

Gunia liliambatanishwa na kuomboleza na huzuni. "Umenisababisha kutokuwa na huzuni tena"

umenivika furaha

Mwandishi anazungumzia furaha kana kwamba ni vazi ambalo linaweza kuvaliwa. "umenisababisha kuwa na furaha"

utukufu wangu utakuimbia wewe sifa

Hapa "utukufu wangu" unamaanisha nafsi ya mwandishi au moyo wake. Hii inamaanisha mwandishi mzima, anaye mwabudu Mungu kwa sababu amemfanya kuwa na furaha. "nitakuimbia wewe sifa"

Psalms 31

Psalms 31:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Katika wewe Yahwe, ninakukimbilia

Kwenda kwa Yahwe kwa ajili ya ulinzi inazungumziwa kama kumkimbilia. "Naenda kwako Yahwe, kwa ajiliya ulinzi"

usiniache niaibike kamwe

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "usiwaache wengine waniaibishe"

uwe mwamba wangu wa kukimbilia; ngome ya kuniokoa

Mseno "uwe mwamba wangu wa kukimbilia" ni ombi kwa ajili ya ulinzi. Msemo wa pili unawekea mkazo msemo wa kwanza.

mwamba wangu wa kukimbilia

Yahwe anazungumziwa kana kwamba yeye ni mwamba mkubwa ambao utamlinda mwandishi na mashambulio. "kama mwamba mkubwa ambao nitakuwa salama"

ngome ya kuniokoa

Yahwe anazungumziwa kana kwamba yeye ni ngome imara ambayo mwandishi anaweza kulindwa dhidi ya adui zake.

Psalms 31:3

mwamba wangu

Yahwe anazungumziwa kana kwamba ni mwamba mkubwa utakao mlinda mwandishi na shambulio. "kama mwamba mkubwa ambao nitakuwa salama"

ngome yangu

Yahwe anazungumziwa kana kwamba ni ngome imara ambao mwandishi atalindwa kutoka kwa adui zake.

kwa ajili ya jina lako

Katika msemo huu "jina" inamwakilisha Yahwe. "ili jina lako lipewe heshima" au "ili nilikuabudu"

niongoze na unichunge

Maneno "kuongoza" na "kuchunga" yana maana sawa na yana imarisha ombi kwambaYahwe amuongoze. "niongoze pale unapotaka niende"

Ning'oe kutoka kwenye wavu walioficha kwa jili yangu

Mwandishi anazungumziwa kana kwamba ni ndege aliye naswa katika wavu, na kumsubiri Yahwe kumweka huru kutoka kwenye mtego.

wewe ni kimbilio langu

Yahwe anazungumziwa kana kwamba ni sehemu ambayo mwandishi anaweza kujificha kutoka kwa watu wanao mshambulia. "wewe hunilinda daima" au "huwa unanipa ulinzi wakati wote"

Psalms 31:5

Katika mikono yako

Mungu ni roho, lakini hapa anazungumziwa kana kwamba ana mikono. Hapa "mikono yako" inamaansiha matunzo ya Yahwe. "katika matunzo yako"

ninaiweka roho yangu

Hapa "roho yangu" inamaanisha mwandishi. "ninajiweka"

Mungu wa uaminifu

"wewe ni Mungu ninayeweza kumtumaini"

Nawachukia wale wanaotumikia sanamu zisizo na faida

"Sanamu hazina faida. Nawachukia wale wanaoziabudu"

umeona mateso yangu ... ulijua dhiki ya nafsi yangu

Misemo hii miwili inaeleza wazo moja kuwa Mungu anajua kuhusu taabu za mwandishi.

dhiki ya nafsi yangu

Hapa "nafsi yangu" inamaani mwandishi. "dhiki yangu"

Psalms 31:8

Umeweka miguu yangu

Hapa "miguu yangu" inamaanisha mwandishi. "Umeniweka"

sehemu ya wazi pana

Waebrania waliona sehemu za wazi pana kama sitiari ya usalama na uhuru. "sehemu ambayo niko huru"

niko katika dhiki

"ninateseka sana"

nafsi yangu na mwili wangu

Maneno "nafsi" na "mwili" yanatumika kumwelezea mtu kamili.

Psalms 31:10

Kwa kuwa maisha yangu yamechoshwa

Hapa "maisha yangu" inamaanisha mwandishi. "Nimekuwa mnyonge sana"

na huzuni ... kwa kugumia

"kwa sababu ya huzuni yangu ... kwa sababu ya kugumia kwangu"

miaka yangu kwa kugumia

Msemo "kuchoka" haumo, ila unadokezwa. "miaka yangu imechoshwa kwa kugumia"

Nguvu yangu inashindwa

Hapa "Nguvu yangu" inamaanisha mwandishi. "Nimekuwa mnyonge"

mifupa yanguinapotea

Hapa "mifupa" inamaanisha afya ya kimwili ya mwandishi. "afya yangu inashindikana"

watu wananidharau

"watu wananitukana"

wanatishwa na hali yangu

"wanashtushwa na hali yangu"

Psalms 31:12

kama mtu mfu ambaye hakuna mtu

Mwandishi anasema kuwa watu wamemsahau sana hadi inakuwa kana kwamba ameshakufa tayari.

kama chungu kilicho vunjika

Mwandishi anajizungumzia kana kwamba hafai kabisa. "sifai kama chungu kilichovunjika"

kunong'ona kwa wengi

Inadokezwa kuwa "wengi" inamaanisha watu. "watu wengi wananisema"

habari za kuogofya kutoka kila upande

"taarifa za kutisha kutoka vyanzo vingi"

kuchukua maisha yangu

Lahaja hii inamaanisha kuua mtu. "kuniua"

Psalms 31:14

Hatima yangu iko mkononi mwako

Hapa "mkononi mwako" inamaanisha nguvu ya Yahwe. "Una nguvu ya kuamua hatima yangu"

wale wanaonifuatilia

"kutoka kwa watu wanaojaribu kunishika"

Fanya uso wako ung'ae kwa mtumishi wako

Mwandishi anamzungumzia Yahwe kumtendea kwa fadhila kana kwamba uso wa Yahwe unang'aa mwanga juu yake. "Tenda kwa fadhili kwa mtumishi wako"

Psalms 31:17

Usiniache niaibike

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Usiwaache wengine wanifanye nijisikie aibu"

Na waovu waaibike!

"Natamani kwamba Mungu awaaibishe watu waovu!"

waovu

Hii inamaanisha watu waovu.

Na wawe kimya kuzimu. Midomo ya uongo inyamazishwe

Wazo hili linarudiwa kusisitiza hamu ya mwandishi kwamba sauti za waovu hazisikiwi.

Na wawe kimya kuzimu

Hapa "kuzimu" inawakilisha kifo. "Acha wafe ili wasiweze kuzungumza"

Midomo ya uongo

Hii inawakilisha watu waongo. "watu wanaodanganya"

inayozungumza dhidi ya wenye haki kwa ujasiri

"wanaosema mambo mabaya kuhusu watu wenye haki"

kwa dharau na kubeza

Maneno haya yana maana ya kufanana. "na dharau sana"

Psalms 31:19

Wema wako

Hii inaweza kuelezwa kama kitenzi. "ni vitu vizuri unavyofanya"

uliutunza

Wema wa Yahwe unazungumziwa kana kwamba ni kitu kinachoweza kutunzwa kama mazao. "unayoweka tayari kwa ajili ya matumizi"

wale wanao kuheshimu

"wale wanao kuheshimu sana"

wanao kukimbilia

Kwenda kwa Yahwe kwa ajili ya ulinzi inazungumziwa kama kumkimbilia. "wale wanaoenda kwako kwa ajili ya ulinzi"

Katika kivuli cha uwepo wako; unawaficha... Unawaficha katika kivuli

Misemo hii miwili inamaanisha kuwa Mungu anawalinda.

katika kivuli

Uwepo wa Yahwe unazungumziwa kana kwamba ni jengo imara ambapo mwandishi atakuwa salama.

Unawaficha katika kivuli

Hapa "kivuli" kinawakilisha sehemu salama. "Unatoa sehemu salama kwa ajili yao"

dhidi ya vurugu ya ndimi

Hapa "ndimi" zinawakilisha watu wanaozungumza mambo makali sana dhidi ya mwandishi. "ambapo adui zao hawawezi kuzungumza uovu kwao"

Psalms 31:21

Nimekataliwa kutoka machoni pako

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Umenitoa katika uwepo wako"

machoni pako

Hapa "macho" yanamaanisha uwepo wa Yahwe. "uwepo wako"

ulisikia ombi langu la msaada

Hapa "ombi" linaweza kuelezwa na kitenzi. "ulinisikia nikiomba msaada"

Psalms 31:23

waaminifu

Hii inamaanisha watu waaminifu. "watu walio waaminifu"

huwalipa wenye kiburi kikamilifu

Hapa "kulipa" ni lahaja inayomaanisha kuwaadhibu. "anawapa watu wenye kiburi adhabu yote wanayostahili"

Psalms 32

Psalms 32:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Maschili

Hii inaweza kumaanisha mtindo wa muziki.

ambaye makosa yake yamesamehewa, ambaye dhambi zake zimefunikwa

Misemo hii ina maana ya kufanana. Inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "ambaye Mungu husamehe makosa yake na kufunika dhambi zake"

dhambi zake zimefunikwa

Hapa dhambi iliyosamehewa inazungumziwa kana kwamba imefunikwa ili isionekane. "ambaye dhambi yake haijaliwi" au "ambaye dhambi yake inasahauliwa makusudi"

ambaye Yahwe hamhesabii hatia

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "ambaye Yahwe anaona hana hatia" au "ambaye hana hatia kulingana na Yahwe"

ambaye rohoni mwake hakuna hila

Hapa "roho" inamaanisha mtu. "ambaye hakuna hila" au "ambaye ni mkweli kabisa"

Psalms 32:3

mifupa yangu ilikuwa inachakaa

Hapa "mifupa yangu" inamaanisha mwandishi. "nilikuwa nachakaa" au "nilikuwa nakuwa mdhaifu"

siku nzima

Lahaja hii inamaanisha "endelevu." "wakati wote"

mchana na usiku

Tofauti hizi zinajumlisha kila kitu katikati. "wakati wote"

mkono wako ulikuwa mzito juu yangu

Hapa "mkono" inamaanisha Yahwe. Msemo wote ni lahaja inayomaanisha "umenitesa." "umenifanya niteseke sana"

Nguvu yangu ilinyauka kama kwenye ukame wa majira ya joto

Nguvu ya Daudi inalinganishwa na mmea mdogo wa kijani unaogeuka kuwa wa rangi ya kahawia na kuanguka katika majira ya kiangazi.

Sela

Hili linaweza kuwa neno la kimuziki linalowaongoza watu jinsi ya kuimba au kujecheza vyombo hapa. Tafsiri zingine huandika neno hili la Kihebrabia, na zingine haziliweki.

Psalms 32:5

Sela

Hili linaweza kuwa neno la kimuziki linalowaongoza watu jinsi ya kuimba au kujecheza vyombo hapa. Tafsiri zingine huandika neno hili la Kiebrania, na zingine haziliweki.

katika kipindi cha dhiki kuu

"wakati wako katika taabu kubwa"

Kisha maji yakifurika, hayatawafikia hao watu

Matatizo yanazungumziwa kana kwamba ni mafuriko ya maji. "Kisha matatizo yatakapokuja kama mafuriko ya maji, watu hao watakuwa salama"

Psalms 32:7

Wewe ni maficho yangu

Yahwe anazungumziwa kana kwamba ni sehemu salama dhidi ya mashambulizi ya adui wa mwandishi. "Wewe ni kama sehemu ambayo naweza kujificha dhidi ya adui zangu"

Utanizunguka na wimbo wa ushindi

Sitiari hii inamaanisha kuwa ulinzi wa Yahwe kwa mwandishi ndio sababu ya nyimbo za ushindi alizoimba. "Kwa sababu yako nitaimba nyimbo za ushindi"

Sela

Hili linaweza kuwa neno la kimuziki linalowaongoza watu jinsi ya kuimba au kujecheza vyombo hapa. Tafsiri zingine huandika neno hili la Kihebrabia, na zingine haziliweki.

Nitakuelekeza na kukufundisha katika njia

Maneno "kuelekeza" na "kufundisha" zinamaana sawa na zinasisitiza maelekezo makini. "Nitakufundisha kila kitu kuhusu njia"

Nitakuelekeza

Hapa anayesema hivi ni Yahwe akimwambia Daudi.

katika njia unayopaswa kwenda

Kuishi katika njia sahihi inazungumziwa kana kwamba ni njia ambayo mwandishi anapaswa kutembea. "jinsi ya kuishi maisha yako"

na jicho langu juu yako

Hapa "jicho langu" linamaanisha Yahwe kuzangatia kwa umakini. "na kuweka umakini wangu kwako" au "kukuangalia"

Psalms 32:9

Usiwe kama farasi ... hawana uelewa

Mwandishi anawafananisha watu wasio na uelewa na farasi au nyumbu. Maana zinazowezekana ni 1) mwandishi anazungumza maneno ya Yahwe kwa wasomaji wake, "Mnapaswa wote kutokuwa kama farasi ... hawana uelewa" au2) Yahwe anazungumza na mwandishi kana kwamba ni kundi la watu.

hatamu na lijamu

Vifaa viwili vinavyotumiwa na watu kuwaongoza farasi na nyumbu kwenda anapotaka mtu.

unapotaka

"popote mtu anapotaka waende."

zitamzunguka

Uaminifu wa Yahwe "utakaomzunguka" unasababisha ulinzi na uongozo."zitamwongoza" au "zitamlinda"

Psalms 32:11

Furahi katika Yahwe

Hapa "katika Yahwe" inamaanisha kile ambacho Yahwe aliwatendea. "Uwe na furaha kwa sababu ya kile ambacho amefanya Yahwe"

wenye haki

Hii inamaanisha watu. "watu wako watakatifu"

piga kelele ya furaha

"piga kelele kwa furaha" au "piga kelele kwa sababu ya furaha"

walio wanyofu moyoni

Hapa "moyo" inamaanisha mtu. "watu walio wanyofu"

Psalms 33

Psalms 33:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Furahi katika Yahwe

Hapa "katika Yahwe" inamaanisha kile ambacho Yahwe aliwatendea. "Furahini kwa sababu ya kile ambacho amefanya Yahwe"

kusifu kunawafaa wanyofu

"kumsifu Yahwe kunafaa kwa watu walio wanyofu"

Psalms 33:4

Taarifa ya Jumla:

Kila mstari una mistari miwili yenye maana za kufanana.

Neno la Yahwe ni imara

Hapa "imara" ni sitiari kwa jambo lililo la kweli. "Yahwe daima hufanya anachosema atafanya"

Anapenda haki na hukumu

Nomino hizi dhahania zinaweza kuelezwa kama vitendo. "Anapenda kufanya kilicho cha haki na sawa" au "Anawapenda wale wanaofanya kilicho cha haki na sawa"

Dunia imejaa uaminifu wa agano la Yahwe

Hapa "Dunia imejaa" ni lahaja inayomaanisha kwamba uaminifu wa agano unaweza kuonekana duniani kote. "Uaminifu wa agano la Yahwe unaweza kupitia duniani kote"

Kwa neno la Yahwe mbingu ziliumbwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Kwa kutumia neno lake, Yahwe aliziumba mbingu"

kwa pumzi ya mdomo wake

Hii inamaanisha neno la Yahwe. "kwa neno lake"

Psalms 33:7

Taarifa ya Jumla:

Kila mstari una mistari miwili yenye maana za kufanana.

kama rundo

"kama nyuma ya bwawa." Mwandishi anaelezea uumbaji wa bahari kana kwamba Mungu anarundika maji yote pamoja.

anaweka bahari katika ghala

Mwandishi anaelezea uumbaji wa bahari kana kwamba Mungu anayaweka katika ghala. "anaweka bahari katika sehemu yake, kama mtu anayeweka mbegu katika ghala"

Acha dunia yote

Hii inamaanisha watu wa duniani. "Acha kila mtu duniani"

isimame kwa kumstaajabu yeye

Hapa "isimame kwa kumstaajabu" ni lahaja inayomaanisha "kustaajabu." "kumheshimu"

ikasimama

Hapa "ikasimama" ni lahaja inayomaanisha "iliumbwa." "kuanza kuwepo"

Psalms 33:10

Taarifa ya Jumla:

Kila mstari una mistari miwili yenye maana za kufanana.

Yahwe huzuia

"Yahwe huangamiza" au "Yahwe huvunja"

mwungano wa mataifa

Hapa "mataifa" yanamaanisha watu wa mataifa haya. "mwungano wa watu wa mataifa tofauti"

mwungano

Mwungano ni makubaliano kati ya mataifa mawili au zaidi kusaidiana katika vita dhidi ya adui mmoja.

mipango ya watu

"dhamira ya watu" "mipango ya uovu ya watu"

inasimama milele

Hapa "kusimama" ni lahaja inayomaanisha "kudumu."

mipango ya moyo wake kwa vizazi vyote

Neno ambalo halipo "kusimama" linadokezwa. "mipango ya moyo wake inasimama vizazi vyote"

mipango ya moyo wake

Hapa "moyo wake" inamaanisha Yahwe. "mipango yake"

kwa vizazi vyote

"kwa vizazi vyote vya mbeleni." Hii ni lahaja inayomaanisha "milele"

Limebarikiwa taifa

Hapa "taifa" linamaanisha watu wa taifa hilo. "Wamebarikiwa watu wa taifa"

ambalo Yahwe ni Mungu wake

"wanao mwabudu Yahwe kama Mungu"

kama urithi wake

Watu ambao Yahwe amewachagua kumwabudu wanaelezwa hapa kana kwamba ni urithi ulioupokea.

Psalms 33:13

anatazama chini

Sehemu ambayo Yahwe huishi inazungumziwa kana kwamba iko juu ya dunia wanayoishi watu.

anyeunda mioyo yao wote

Hapa "mioyo" inamaanisha kuwaza kwa hawa watu. Mwandishi anamzungumzia Yahwe kuongoza kufikiri kwa watu kana kwamba alikuwa ni mfinyanzi anayeunda bakuli. "huongoza mawazo yao kama mfinyanzi anavyounda bakuli"

Psalms 33:16

Hakuna mfalme anayeokolewa kwa jeshi kubwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Jeshi kubwa sicho kinachomwokoa mfalme"

Farasi ni usalama wa uongo

Hapa "farasi" inawakilisha sehemu yenye nguvu zaidi ya jeshi. "Kuwa na jeshi lenye farasi imara halitoi usalama"

Psalms 33:18

Tazama

Neno hili linaonesha kuwa wazo jipya linaanza katika zaburi hii. "Angalia" au "Sikiliza" au "Zingatia ninachotaka kukuambia"

jicho la Yahwe

Hapa "jicho" linamaanisha umakini au usikivu wa Yahwe. "Usikivu wa Yahwe"

wanao tegemea

"wanaosubiri" au "wanaotumaini"

kuokoa maisha yao na mauti

Hapa "maisha yao" inamaanisha watu. "kuwaepusha na kufa"

Psalms 33:20

Tunamsubiri Yahwe

"Kusubiri" hapa ni lahaja inayomaanisha kutumaini. "Tunamwamini Yahwe" au "Tunamtumaini Yahwe"

yeye ni msaada wetu na ngao yetu

Hapa Yahwe anazungumziwa kana kwamba ni ngao inayowalinda askari vitani. "yeye ni msaada wetu na hutulinda kama ngao"

Mioyo yetu inafurahi

Hapa "mioyo" inamaanisha watu. "Tunafurahi"

katika jina lake takatifu

Hapa "jina takatifu" linamaanisha tabia takatifu ya Yahwe. "katika tabia yake takatifu" au "katika yeye kwa sababu ni mtakatifu"

Psalms 33:22

kuwa nasi

Lahaja hii inamaanisha "tusaidie." "tenda kwa faida yetu" au "tusaidie" au "tulinde"

tunapoweka tumaini letu kwako

"tunapotumaini msaada wako"

Psalms 34

Psalms 34:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

kujifanya kuwa mwenye wazimu

"kuigiza kama mtu chizi"

mbele ya Abimeleki

Hii inamaanisha tukio bayana la kihistoria ambalo Wahebrania wanafahamu vizuri. "alipokuwa katika nyumba ya Abimeleki" au "alipokuwa mfungwa wa Abimeleki"

mfukuza

"mwondoa kwa nguvu"

sifa yake daima itakuwa mdomoni mwangu

Hapa "mdomoni mwangu" inamaanisha Daudi kumzungumzia Mungu. "daima nitamsifu kwa sauti"

Psalms 34:2

walio kandamizwa

Hii inamaanisha watu walio kandamizwa. "watu walio kandamizwa"

Msifuni Yahwe pamoja na mimi

Kitenzi "msifuni" ni amri kwa kikundi. "Kila mtu anapaswa kumsifu Yahwe pamoja na mimi"

inueni jina lake

Hapa "inueni" ni lahaja inayomaanisha kumtukuza Yahwe. "waambieni watu jinsi alivyo mkuu"

jina lake

Hapa "jina lake" linammanisha tabia ya Yahwe. "tabia yake"

Psalms 34:4

Nilimtafuta Yahwe

Hapa "Nilimtafuta Yahwe" inamaanisha kuwa Daudi alikuwa akimwomba Yahwe msaada. "Niliomba kwa Yahwe" au "Nilimwomba Yahwe msaada"

Wale wanaomtazama

Hapa "wanaomtazama" inawakilisha kutafuta msaada kutoka kwake. "Wale wanaomtazama yeye kwa ajili ya msaada" au "wale wanaotegemea msaada kutoka kwake pekee"

wanang'aa

Lahaja hii inamaanisha mwonekano wao kuwa wa furaha. "wana furaha"

nyuso zao hazina aibu

Hapa "nyuso zao" inamaanisha watu wanaomtazama Yahwe. Inaweza pia kuelezwa katika hali chanya. "hawana aibu" au "wana majivuno"

Mtu huyu aliye kandamizwa

Daudi anajieleza kama mtu aliye kandamizwa. "Nilikandamizwa na"

Yahwe akamsikia

Hapa "kusikia" inamaana kuwa Yahwe alimsaidia. "Yahwe alinisikia" au "Yahwe alinisaidia"

Psalms 34:7

huzungusha kambi

Malaika wa Yahwe anazungumziwa kana kwamba alikuw ani jeshi linalozungusha kambi kwa mtu ili kuwalinda. "hulinda"

Onjeni mwone Yahwe yu mwema

Wema wa Yahwe unazungumziwa kana kwamba ni kitu kinachoweza kuonjwa na kuonwa. "Jaribuni na mwone kuwa Yahwe ni mwema"

anaye mkimbilia

Yahwe anazungumziwa kana kwamba ni sehemu ambayo watu wanaweza kujificha kwa ajili ya ulinzi kutoka kwa adui zao. "mwamini kuwalinda"

Hakuna upungufu kwa wale wanaomcha yeye

Hii inaweza kuelezwa katika hali chanya. "Wale wanaomcha daima watakuwa na kile wanachohitaji"

Psalms 34:10

hawatapungukiwa chochote kizuri

Hii inaweza kuelezwa katika hali chanya. "daima watakuwa na vitu vizuri wanavyohitaji"

wana

Hapa hii haimaanishi wana wa mwandishi halisi, lakini watu anaowafundisha kuhusu Yahwe. "wanafunzi wangu"

Psalms 34:12

Kuna mtu gani anayetamani maisha na kupenda siku nyingi, ili aone mema?

Jibu linalodokezwa la swali hili ni "kila mtu." Swali hili balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Kila mtu anatamani maisha na anatamani kuishi siku nyingi na kuwa na maisha mazuri"

weka ulimi wako mbali na uovu ... weka midomo yako mbali na kuongea uongo

Misemo hii miwili inamaanisha kitu kimoja na inasemwa katika njia tofauti ili kusisitiza umuhimu wake.

Basi weka ulimi wako mbali na uovu

Hapa "ulimi" inamaanisha mtu mzima. "Basi, usizungumze uongo"

weka midomo yako mbali na kuongea uongo

Hapa "midomo" inamaanisha mtu anayezungumza. "usizungumze uongo"

Ugeuke uovu

Hapa "ugeuke" ni sitiari ya kuepuka na uovu. "Kataa kufanya uovu"

Tafuta amani

Hapa "kutafuta" inamaanisha kujihusisha na amani. "Jaribu kwa bidii kuishi kwa amani na watu wengine"

Psalms 34:15

Macho ya Yahwe yako juu ya wenye haki

Hapa "macho ya Yahwe" inamaanisha kutazama kwake kwa makini. "wenye haki" inamaanisha watu wenye haki. "Yahwe huwatazama kwa makini watu wenye haki"

mskio yake yameelekezwa kwa kilio chao

Hapa "maskio yake" inamaanisha hamu ya Yahwe kuwajibu. "anazingatia kilio chao" au "anajibu kilio chao"

kukata kumbukumbu yao duniani

Yahwe atawasababisha watu wawasahau kabisa watakapokufa hadi inakuwa kana kwamba ametumia kisu kuikata kumbukumbu yao. "ili watakapokufa, watu watawasahau kabisa"

Yahwe husikia

Hapa "husikia" inamaanisha kuwa Yahwe anatamani kuwajibu. "Yahwe anawazingatia"

Psalms 34:18

Yahwe yuko karibu

Hapa "yuko karibu" inamaana "tayari kusaidia." "Yahwe yuko tayari kusaidia"

walio vunjika moyo

Huzuni kubwa inazungumziwa kana kwamba moyo wa mtu umevunjika. "watu walio na huzuni sana"

wale walio pondeka rohoni

Watu waliokata tamaa sana wanazungumziwa kana kwamba roho zao zimepondwa. "watu waliokata tamaa sana"

wenye haki

Hii inamaanisha watu wenye haki. "watu wenye haki"

Anatunza mifupa yake yote, hakuna hata moja itakayovunjika

Hapa "mifupa yake" ni halisia, lakini pia inaashiria kuwa yahwe anamtunza mtu mzima. "Anatoa ulinzi kamili kwake, hatadhuriwa kwa njia yoyote"

Psalms 34:21

Uovu utawaua waovu

Uovu unazungumziwa kana kwamba mtu anayeweza kuua watu. "Matendo maovu ya watu waovu yatawaua"

waovu

Hii inamaanisha watu waovu.

Wale wanaowachukia wenye haki watahukumiwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe atawahukumu wale wanaowachukia wenye haki"

wenye haki

Hii inamaanisha watu wenye haki.

Hakuna atakaye hukumiwa kwa wanaomkimbilia

Hii inaweza kutafsiriwa katika hali ya kutenda. Inaweza pia kutafsiriwa katika hali chanya. "Yahwe atawasamehe wote wanaomkimbilia"

wanaomkimbilia

Kwenda kwa Yahwe kwa ajili ya ulinzi inazungumziwa kama kumkimbilia. 'kwenda kwake kwa ajilil ya ulinzi"

Psalms 35

Psalms 35:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Kamata ngao yako ndogo na ngao kubwa ... mkuki wako na shoka ya vita

Misemo hii inamwelezea Mungu kama shujaa ambaye anajiandaa kwa ajili ya vita.

ngao yako ndogo na ngao kubw

hizi ni silaha za kujilinda

mkuki wako na shoka ya vita

hizi ni silaha za mashambulizi

wale wanaonifukuza

Maana zinawezekana ni 1) hawa ni adui wanaomfukuza mwandishi kiuhalisia au 2) hii ni sitiari ya watu ambao ni adui wa mwandishi.

sema kwa nafsi yangu

Hii inamaanisha mwandishi. "sema kwangu"

Mimi ni wokovu wako

"Mimi ni mwokozi wako" au "Nitakuokoa"

Psalms 35:4

Na wale wanaotafuta maisha yangu waaibike na kunyimwa heshima

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Na Yahwe awaaibishe na kuwanyima heshima wale wanaotafuta maisha yangu"

Na

"Natamani kwamba"

wanaotafuta maisha yangu

Hapa "maisha yangu" inamaana wanatamani kumuua mwandishi. "wanaojaribu kuniua"

Na wale wanaopanga kunidhuru wageuzwe na washangazwe

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Na Yahwe awageuze na kuwashangaza wale wanaopanga kunidhuru"

wageuzwe

"wageuzwe" ni sitiari ya kushindwa kutimiza lengo lao. "kushindwa kufanikiwa"

washangazwe

"wachanganyikiwe" au "kuwafadhaisha"

kama makapi mbele ya upepo

Adui wa mwandishi wanazungumziwa kana kwamba ni nyasi ambayo inapulizwa kwa urahisi. "kupulizwa na upepo kama makapi"

njia yao

Hapa "njia yao" inamaanisha maisha yao. "maisha yao"

giza na utelezi

Hii inamaanisha njia iliyojificha na hatari. "imejificha na imejaa hatari"

anawafukuza

Hii inamaanisha malaika wa Yahwe kuwa kinyume na adui wa mwandishi. "anaenda kinyume nao" au "anawapinga"

Psalms 35:7

wanaliandaa wavu wao kwa ajili yangu

Njama za waovu zinazungumziwa kana kwamba ni wavu walioweka kumnasa mwandishi.

walichimba shimo kwa ajili ya maisha yangu

Njama za waovu zinazungumziwa kana kwamba ni shimo walilochimba kumkamata mwandishi. "walitaka kunishika katika shimo kama mnyama mkubwa"

maisha yangu

Hii inamaanisha mwandishi. "mimi"

Acha maangamizi yawapite kwa kushtukiza

Maangamizi yanazungumziwa kana kwamba ni mnyama hatari ambaye atawavamia ghafla. "Acha waangamizwe ghafla" au "Acha washtukizwe kwa sababu umewaangamiza ghafla"

wavu waliouandaa

Njama za waovu zinazungumziwa kana kwamba zilikuwa ni wavu walioweka kumnasa mwandishi. "wavu walioweka ili kuninasa kama mnyama na kunidhuru"

Acha waanguke humo

Hii ni sitiari kama mstari wa 7. Wavu umekusudiwa kumnasa mwandishi. "Acha waanguke katika shimo walilo nichimbia"

waanguke humo

Maana zinazowezekana ni 1) kuanguka katika shimo la mstari wa 7 au 2) kuanguka katika uharibifu.

maangamizi yao

"ili waangamizwe" au "hivyo ndivyo unavyopaswa kuwaangamiza"

Psalms 35:9

katika wokovu wake

Nomino dhahania "wokovu" inaweza kuelezwa kama kitenzi. "kwa kuwa umeniokoa"

Mifupa yangu yote

Hapa "mifupa" inamaanisha undani zaidi wa mtu. "Undani wangu wote"

Yahwe, ni nani aliye kama wewe ... wale wanao jaribu kuwaibia?

Jibu linalodokezwa kwa hili swali ni kwamba hakuna aliye kama Yahwe. "Yahwe, hakuna aliye kama wewe ... wale wanaojaribu kuwaibia"

maskini na wahitaji

Maneno "maskini" na "wahitaji" yana maana ya kufanana na yanasisitiza kuwa Yahwe anawaokoa wengi wanaohitaji msaada wake.

Psalms 35:11

inuka

Hii inamaanisha kuwa wanashuhudia katika majaribu. "kujitolea kutoa ushuhuda"

Wananilipa maovu kwa mema

Hii ni sitiari inayomaanisha wanarudisha marejeo maovu kwa mema waliyopokea. "Kwa kunirudishia kutenda wema wangu, wanafanya vitu viovu kwangu"

maovu ... mema

Nomino dhahania hizi zinaweza kuelezwa katika hali zingine. "vitu viovu ... vitu vizuri"

Nina huzuni

"Nina huzuni sana"

Psalms 35:13

walipokuwa wagonjwa

Wagonjwa hapa inamaanisha "mashahidi waovu"

Nilivaa gunia

"Nilionesha kuwa nina huzuni"

na kichwa changu kikiwa kimeinamishwa kifuani mwangu

Hii ilikuwa ishara ya maombi. "na kichwa changu kimeinama chini katika maombi"

katika majonzi kama kwa ndugu yangu

Mwandishi alikuwa na huzuni kana kwamba ndugu yangu amekufa. "kuhuzunika kana kwamba ndugu yangu mwenyewe alikuwa ameugua"

Niliinama katika kuomboleza kama kwa mama yangu

Mwandishi aliomboleza kana kwamba mama yake amekufa. "Niliomboleza kana kwambamama yangu amekufa"

Niliinama

Hii ilikuwa alama ya maumivu na mateso.

Psalms 35:15

wakakusanya pamoja

"kukusanyika pamoja" au "wakaja pamoja"

dhidi yangu

Hii inamaanisha walikuja pamoja kwa kusudi la kumshambulia mwandishi. "kufanya mipango dhidi yangu" au "kupanga uharibifu"

Wakanirarua

Hapa walimtendea mwandishi kana kwamba alikuwa kipande cha nguo walichoweza kurarua vipande vipande. "Walinivamia"

Bila heshima yoyote wakanidhihaki

"Walinidhihaki na watu wasio na faida kabisa" au 2) "walinikejeli bila heshima"

wakanisagia meno

Hii ni alama ya hasira na chuki. "walinifanyia sauti za kusaga kwa meno yao"

Psalms 35:17

hadi lini utanitazama?

Hili swali la balgha linaashiria kuwa mwandishi anamtaka Mungu kuacha tu kumtazama na kuanza kumsaidia. "hadi lini utawatazama tu wakifanya hivi" au "utanisaidia lini"

Okoa nafsi yangu

Hapa "nafsi" inamaanisha mwandishi. "Niokoe"

maisha yangu kutoka kwa simba

Neno "okoa" linadokezwa. "okoa maisha yangu kutoka kwa simba"

maisha yangu

Hii inamaanisha mwandishi. "mimi"

kutoka kwa simba

Hapa mwandishi anazungumzia adui zake kana kwamba ni simba wakali. "kutoka kwa adui zangu wanaonivamia kama wanyama pori"

Psalms 35:19

Usiache adui zangu waongo

"Usiache adui zangu, wanaosema uongo kunihusu,"

njama zao za uovu

"mipango yao ya uovu"

hawazungumzi amani

"hawazungumzi kwa amani na watu"

kupanga maneno ya uongo

"wanatafuta njia za kusema uongo"

wale katika nchi yetu wanao ishi kwa amani

"wale wanaoishi kwa amani katika nchi yetu"

ishi kwa amani

"usimdhuru yeyote"

Psalms 35:21

Wanafungua midomo wazi yao dhidi yangu

Sababu ya kufungua midomo yao ni kumshtaki mwandishi. "Wananipigia kelele ili wanashtaki"

Aha, Aha

Huu ni mshangao unaotumika wakati kitu kinaonekana ghafla au kueleweka. Unaweka mkazo katika kauli inayofuata.

macho yetu yameona

Hapa "macho yetu" inamanisha macho ya adui. Inadokezwa kuwa wanasema kwamba wamemwona mwandishi anafanya kitu kibaya. "tumeona" au "tumeona makosa uliyofanya"

Umeiona

Hapa walichoona ni mashtaka ya uongo ya adui wa mwandishi. "Umeona jinsi walivyonishtaki kimakosa"

usiwe kimya

"usiache kujali walichonifanyia." Hii inaweza kuelezwa katika hali chanya. "wahukumu kwa sababu ya kile walichofanya"

usiwe mbali na mimi

Hii inaweza kuelezwa katika hali chanya. "uwe karibu sana na mimi"

Jiinue na uamke

Hii haimaanishi kuwa Mungu kweli yuko usingizi. Mwandishi anataka Mungu aingilie kati. Maneno yote yana maana moja na yanasisitiza uharaka wa ombi hili. "Nahisi kama umelala! Amka"

kwa utetezi wangu

"kunilinda"

madai yangu

Hii inamaanisha mwandishi. "mimi"

Psalms 35:24

usiwaache wafurahi juu yangu

"usiwaache wafurahi kwa sababu ninateseka"

waseme moyoni mwao

Hii ni lahaja inayomaanisha kujisemesha. "wajisemeshe"

Aha

Huu ni mshangao unaotumika wakati kitu kinaonekana ghafla au kueleweka. Unaweka mkazo katika kauli inayofuata. "Ndio"

tumepata tunalichokuwa tunataka

Inadokezwa kuwa adui wa mwandishi walitaka atangazwe kuwa na hatia. "ametangazwa kuwa na hatia kama tulivyokuwa tunatamani!"

Tumemmeza

Adui wa mwandishi wanazungumzia uharibifu wake kana kwamba waoni wanyama pori waliommeza. "Tumemwangamiza"

shangaze

"aibishe" au "fadhaishe"

Na wale wanao nidhihaki wafunikwe na aibu na kukosa heshima

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Na uwafunike kwa aibu na kukosa heshima wale wanao nidhihaki"

nidhihaki

kumtukana mtu ili kumkasirisha

wafunikwe na aibu na kukosa heshima

Hapa aibu na kukosa heshima zinazungumziwa kana kwamba zilikuwa nguo za aibu ambazo mwandishi aliweza kuvaa. Nomini dhahania hizi zinaweza kuelezwa kama vitenzi. "waaibishwe na kukosa heshima"

aibu na kukosa heshima

Haya maneno yana maana za kukaribiana na yanatumika kuonesha ni kiasa gani watashushwa.

Psalms 35:27

uthibitisho wangu

Hapa "uthibitisho" unamaanisha Yahwe kumtangaza au kumhukumu mwandishi wa zaburi kuwa hana hatia.

na waseme kwa kuendelea

"na daima waseme"

Yahwe asifiwe

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Acha tumsifu Yahwe"

anaye furahi katika

"anayefurahishwa na" au "anayefurahishwa kwa"

ustawi

hali njema, furaha

sema kuhusu haki yako

"kutangaza kuwa unatenda yaliyo sawa"

Psalms 36

Psalms 36:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Zaburi ya Daudi mtumishi wa Yahwe

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Dhambi inazungumza kama mwaguzi

Dhambi inaelezwa kana kwamba ni nabii wa uongo. "Dhambi ni kama nabii wa uongo anayezungumza"

katika moyo wa mtu mwovu

Hapa "moyo" inamaanisha hali ya ndani wa mtu. "hali ya ndani ya mtu mwovu"

mtu mwovu

Hii haimaanishi mtu bayana, lakini kwa watu waovu kwa ujumla. "watu waovu"

katika macho yake

Hapa "macho" yanamaanisha mtu mwovu. "ndani yake"

anajifariji, akifikiri

"anapendelea kuamini" au "anataka kufikiri"

dhambi yake haitagunduliwa na kuchukiwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Mungu hatagundua na kuchukia dhambi yake"

Psalms 36:3

Maneno yake ni

Hii inamaanisha kauli zake. "Anachosema ni"

kufanya mema

"kufanya vitu ambavyo ni vyema"

anaenda katika njia ya uovu

Vitendo vya dambi vyamtu vinazungumziwa kana kwamba alikuwa akitembea kwenye njia ambayo ilikuwa na uovu.

hapingi uovu

"hapingi tabia za uovu"

Psalms 36:5

unafika mbinguni

Ukuu wa uaminifu wa Mungu wa agano unazungmziwa kana kwamba uko juu sana. "uko juu kama mbingu" au "ni mkuu sana"

unafika kwenye mawingu

Ukuu wa uaminifu wa Mungu unazungumziwa kana kwamba uko juu sana. "uko juu kama mawingu" au "ni mkuu sana"

kama milima ya Mungu ... kama kina kirefu

Misemo hii inaeleza ukuu wa haki ya Mungu na hukumu zake kana kwambazilikuwa juu zana na zenye kina kirefu. "juu kama mlima ya juu zaidi ... mrefu kama bahari lenye kina kirefu zaidi"

unatunza

"unasaidia" au "unaokoa"

Psalms 36:7

Jinsi ulivyo wa thamani uaminifu wako wa agano

Uaminifu wa Agano wa Mungu unazungumziwa kana kwamba kilikuwa kito adimu na cha gharama. "Uaminifu wako wa agano ni wa thamani kama kito adimu.

Wanadamu hukimbilia

"Watu watatafuta ulinzi"

Wanadamu hukimbilia chini ya kivuli cha mbawa zako

Mungu hana mbawa kweli. Hii ni sitiari ya ulinzi wa Mungu. "Wanadamu hukimbilia kwako kama ndege wadogo wanavyotafuta ulinzi chini ya mbawa za mama yao"

Wataridhishwa tele

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Utawaridhisha tele"

kwa wingi wa chakula katika nyumba yako

Hii haimaanishi kuwa Mung ana nyumba yenye chakula. Hii ni sitiari ya utoaji wa vitu tele. "kana kwamba wanakula chakula kizuri kutoka katika nyumba yako" au "kwa baraka zako nzuri"

utawaacha wanywe kutoka katika mto wa baraka zako za thamani

Kuna sitiari mbili hapa. Baraka tele za Mungu zinazungumziwa kana kwamba ni maji yanayotiririka katika mto. Pia, wale wanaopokea hizo baraka wanazungumziwa kana kwamba wanazinya kama maji. "baraka zako za thamani ni kama mto ambao utawaruhusu wanywe kutokea humo"

chechemi ya uzima

"chanzo cha maisha"

katika nuru yako tunaona nuru

Hapa "nuru" ni sitiari ya maarifa ya kweli. "unapotuelimisha, tutajua ukweli" au "nuru yako ndio inayotuwezesha kujua ukweli kukuhusu"

Psalms 36:10

Endeleza uaminifu wa agano lako kikamilifu

"Endeleza uaminifu wako wa agano"

ulinzi wako kwa wanyofu wa moyo

"Endelea" inadokezwa kutoka katika msemo uliopita. "Endelea kuwalinda wanyofu wa moyo"

wanyofu wa moyo

Hapa "moyo" inamaanisha watu. "wanyofu" au "watu wanaoenenda kwa haki"

mguu wa aliye na majivuno ... mkono wa mwovu

Hapa "mguu" na "mkono" inamaanisha watu waovu. Hawa sio watu bayana. Hii inamaanisha watu waovu kwa ujumla. "watu wenye majivuno ... watu waovu"

uniondoe

"unifanye niondoke sehemu yangu"

watenda maovu wameanguka; wameangushwa chini na hawawezi kuinuka

Misemo hii mitatu inaeleza watenda maovu kama watu walioshindwa.

wameangushwa chini

"umewaangusha chini" au "umewaangamiza"

hawawezi kuinuka

"hawawezi kuinuka"

Psalms 37

Psalms 37:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Usikasirike kwa sababu ya watenda maovu

"Usiwaruhusu watu waovu wakukasirishe" au "Usisumbuliwe na kile ambacho watu waovu wanafanya"

watakauka kama nyasi ... kunyauka kama mimea ya kijani

Watenda maovu wanazungumziwa kana kwamba ni nyazi na mimea iliyokauka na inakufa katika hali ya hewa ya joto. Mifanano hii miwiliyote inamaana kuwa watakufa. "kufa" au "kufika mwisho"

Psalms 37:3

chunga katika uaminifu

Uaminifu unazungumziwa kana kwamba ni mnyama atakepata nguvu kwa kula katika malisho mazuri. "rutubisha uaminifu" au "zidisha uaminifu wako"

hamu zako za moyoni

Hapa "moyo" unawakilisha hali ya ndani ya mtu na mawazo. "hamu zako za ndani" au "vitu unavyotamani zaidi"

Psalms 37:5

Mpe Yahwe njia zako

Hapa "kumpa njia zako" ni lahaja inayomaanisha kumwomba Yahwe kuongoza maisha yako. "Mwombe Yahwe aongoze matendo yako katika maisha"

atatenda kwa niaba yako

Hii ni kumwakilisha mwingine katika mambo ya kisheria. Hapa, mtu anayemtumaini Yahwe, atamlinda mtu huyo na kumpa haki mtu huyo.

kama mchana ... kama siku mchana

Misemo hii yote ina maana ya kufanana.

kama mchana

Hii inamaanisha "mbele ya watu wote." "wazi kuona kama mwanga wa mchana"

kama siku mchana

HIi inamaanisha "kuonekana kama jua la mchana." "kuonekana kama nuru wakati wa mwanga zaidi mchana"

Psalms 37:7

Uwe mtulivu

"Uwe kimya"

Psalms 37:8

watakatwa

Uharibifu wa waovu unazungumziwa kana kwamba walikuwa ni matawi ya mmea uliokatwa na kutupwa.

lakini wale wanaomsubir yahwe

"lakini wale wanaomtumaini Yahwe"

watarithi nchi

Kumiliki nchi kunazungumziwa kana kwamba itapokelewa kama urithi. "watapokea nchi kama urithi wao" au "wataishi kwa usalama katika nchi"

atapotea

Lahaja hii inamaanisha kifo cha mtu mwovu. "atakufa na hautamwona tena"

Psalms 37:11

wapole

Hii inamaanisha watu walio wapole. "watu wapole"

watarithi nchi

Kumiliki nchi kunazungumziwa kana kwamba itapokelewa kama urithi. "watapokea nchi kama urithi wao" au "wataishi kwa usalama katika nchi"

mtu mwovu

Hii haimaanishi mtu bayana. Inamaanisha watu waovu kwa ujumla. "mtu mwovu"

mwenye haki

Hii haimaanishi mtu bayana. Inamaanisha watu wenye haki kwa ujumla. "mtu mwenye haki"

kusaga meno

Mtu mwovu anamchukia mtu mwenye haki sana hadi anasaga meno yake pamoja kuonesha hasira yake.

siku yake inakuja

Inadokezwa kuwa "siku yake" itakuwa siku ya hukumu. "siku inakuja ambapo Yahwe atamhukumu na kumwadhibu" au "siku inakuja ambapo Yahwe atamhukumu na kumwadhibu mtu mwovu"

Psalms 37:14

Waovu

Hii inamaanisha watu waovu. "Watu waovu"

wametoa upanga wao ... wamekunja upinde wao

"Upanga" na "upinde" zote ni silaha zinazotumika kushambulia watu. Kitendo kwamba zimetolewa na kukunjwa inamaanisha kuwa wako tayari kushambulia. "wameandaa silaha zao ili kushambulia"

kuwatupa chini

Uharibifu wa watu wahitaji unazungumziwa kana kwamba ni vyombo vya udongo vinavyoweza kuvunjika katika vipande vikitupwa chini. "kuwaangamiza"

waliokandamizwa na wahitaji

Misemo hii inamaana watu wale wale wasio na uwezo wa kujilinda. "watu wasio weza kuwapinga"

Panga zao zitachoma mioyo yao wenyewe

Panga ni mfano wa silaha na "mioyo" inawakilisha watu. "Kuchoma moyo" ni lahaja inayomaanisha "kuua." "Silaha zao zitageuzwa kwao na watajiua wenyewe"

Psalms 37:16

Bora kidogo alichonacho mwenye haki kuliko kingi cha watu waovu wengi

Hapa mstari wa pili ni tofauti na wa kwanza. "Ni bora kuwa mwenye haki, hata kama inamaanisha utakuwa maskini, kuliko kuwa mwovu na utajiri mkubwa"

Bora kidogo alichonacho mwenye haki

"Ni bora kuwa mwenye haki, hata kama inamaanisha utakuwa maskini"

kidogo

Hii inamaanisha kuwa na mali kidogo.

mwenye haki

Hii inamaanisha mtu mwenye haki. "mtu mwenye haki ana"

kingi

Hii inamaanisha utajiri wa watu waovu.

Kwa kuwa mikono ya watu waovu itavunjwa

Hapa "mikono" inawakilisha nguvu ya watu waovu. Kuvunja mikono yao inawakilisha kuwanyanganya nguvu yao. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Kwa kuwa Yahwe ataondoa uwezo wa watu waovu"

Psalms 37:18

huwaangalia wasio na lawama

"Kuangalia" inamaanisha kumlinda mtu. Hapa 'wasio na lawama" inamaanisha watu wasio na lawama. "huwalinda watu wasio na lawama"

siku kwa siku

"kila siku" au "kwa kuendelea"

wakati nyakati ni mbaya

Msemo huu unamaanisha maafa, kama njaa. "maafa yanapotokea"

Psalms 37:20

Adui wa Yahwe watakuwa kama utukufu wa malisho

Mwandishi analinganisha adui wa Yahwe na maua yanayo chanua katika mashamba.

watateketezwa na kupotea katika moshi

Mwandishi anazungumzia uharibifu wa waovu kwana kwamba ni magugu au maua yaliyo nyauka shambani yanayochomwa baada ya mavuno. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe atawaangamiza kama moto unavyogeuza magugu ya shamba kuwa moshi"

ni mkarimu na hugawa

Hizi zina maana moja na zinasisitiza ukarimu wa wenye haki.

Psalms 37:22

Wale walio barikiwa na Mungu

"Wale ambao Mungu anawabariki"

watarithi nchi

Umiliki wa nchi unazungumziwa kanakwamba umepokelewa kama urithi. "watapokea nchi kama mali yao" au "wataruhusiwa kuishi kwa usalama katika nchi"

wale waliolaaniwa naye

"wale ambao Yahwe amewalaani"

watakatwa

Uharibifu wa watu waovu unazungumziwa kana kwamba ni tawi la mmea uliokatwa na kutupwa.

Ni kupitia Yahwe hatua za mtu zinaimarishwa ... inpendeza machoni pa Mungu

"Kama mtu anaishi katika njia ya kupendeza machono pa Yahwe, Yahwe ataimarisha njia zake"

Ni kupitia Yahwe hatua za mtu zinaimarishwa

"Yahwe ndiye anayemwezesha mtu kufanikiwa"

mtu ... mtu

Hii haimaanishi mtu bayana, lakini kwa watu kwa ujumla.

hatua za mtu

Hatua zinawakilisha jinsi mtu anavyoishi. "jinsi mtu anavyoishi"

Ingawa anajikwaa, hataanguka

Hapa "kujikwaa" na "kuanguka" inamaanisha jinsi mtu anavyojibu katika vipindi vigumu. "Ingawa ana vipindi vigumu, hatashindwa kabisa"

anamshika kwa mkono wake

Hapa "mkono wake" inamaanisha nguvu ya Yahwe, na "kumshika" inamaanisha kumlinda. "kumlinda na nguvu yake"

Psalms 37:25

mtu mwenye haki ameachwa

"Yahwe amwacha mtu mwenye haki"

mtu mwenye

Hii haimaanishi mtu bayana. Ni kauli ya ujumla.

wakiomba mkate

Hapa "mkate" inwakilisha chakula kwa ujumla. "kuomba chakula"

Siku nzima

Lahaja hii inamaanisha tendo hili ni tabia ya maisha yake.

watoto wake wanakuwa baraka

"watoto wanakuwa kuwabariki wengine"

Geuka

Kuacha kufanya kitu inazungumziwa kana kwamba mtu ankigeuka. "Acha kufanya"

Psalms 37:28

Wanatunzwa milele

"Yahwe atawalinda milele"

watakatwa

Uharibifu wa waovu unazungumziwa kana kwamba walikuwa tawi la mmea uliokatwa na kutupwa.

wenye haki

"watu wenye haki"

watarithi nchi

Umiliki wa nchi unazungumziwa kana kwamba umepokelewa kama urithi. "watapokea nchi kama urithi wao" au "wataruhusiwa kuishi katika nchi kwa usalama"

Mdomo wa mtu mwenye haki

Hapa "mdomo" unawakilisha mtu mzima anayezungumza. "Mtu mwenye haki"

huzungumza hekima

"huwapa wengine ushauri wa hekima"

huongeza hukumu

"huwatia moyo watu wengine kuishi kwa haki"

Psalms 37:31

Sheria ya Mungu wake moyoni mwake

Hapa "moyo" unamaanisha hali yake ya ndani zaidi. "Anathamini amri za Mungu wake ndani mwake"

miguu yake haitateleza

Kushindwa kwake kumtii Yahwe kunazungumziwa kama kuteleza kwenye njia salama au kuanguka. "atatembea salama katika njia ambayo Mungu anataka atembee" au "atafanya kwa usalama vitu ambavyo Mungu anataka afanye"

Mtu mwovu ... mtu mwenye haki ... mtu mwovu

Hawa sio watu bayana. Inamaanisha aina hii ya watu kwa ujumla.

humtazama mtu mwenye haki

Hapa kutazama inaashiria kuwaangalia wenye haki ili kuwadhuru. "husibiri ili kumvamia mtu mwenye haki"

mkono wa mtu mwovu

Hapa "mkono" unawakilisha uwezo au nguvu. "uwezo wa mtu mwovu"

anapohukumiwa

Hii inamaanisha Yahwe kumhukumu mtu mwenye haki. "Yahwe atakapomhukumu"

Psalms 37:34

atakuinua kumiliki nchi

Hapa "kuinuka" inamaanisha Mungu kuwapa heshima wale wanaomsubiri. "atakuheshimu kwa kukupa nchi"

waovu

"watu waovu"

wanakatwa

Uharibifu wa waovu unazungumziwa kana kwamba walikuwa tawi la mmea uliokatwa na kutupwa.

Psalms 37:35

waovu na mtu wa kutisha

Hii haimaanishi mtu bayana. Ni kauli ya ujumla.

wanasambaa kama mti wa kijani katika udongo wake wa asili

Hapa mafanikio ya mtu mwovu yanazungumziwa kana kwamba ni mti wenye afya unaoota kwatikaudongo mzuri.

hakupatikana

"Sikuweza kumpata" au "Yahwe alimchukua"

Psalms 37:37

mtu wa uadilifu

Hii haimaanishi mtu bayana. Ni kauli ya ujumla.

mwekee alama mnyofu

"waangalia kwa makini watu wazuri"

siku za usoni za mtu mwovu zimekatwa

"Mungu atasitisha uzao wake" au "hatakuwa na uzao"

siku za usoni

Hii inamaanisha uzao wake. "uzao wake"

mtu mwovu

Hii haimaanishi mtu bayana. Ni kauli ya ujumla.

zimekatwa

Uharibifu wa waovu unazungumziwa kana kwamba walikuwa tawi la mmea uliokatwa na kutupwa.

Psalms 37:39

Wokovu wa wenye haki hutoka kwa Yahwe

"Yahwe huokoa watu wenye haki"

wenye haki

"watu wenye haki"

huwasaidia ... huwaokoa ... huwaokoa

Wazo hilo hilo linarudiwa kwa njia tofauti kusisitiza kuwa Yahwe ni wa kutegemewa na anaweza kutoa msaada.

wamemkimbilia

Kwenda kwa Yahwe kunazungumziwa kama kumkimbilia. "wameenda kwake kwa ajili ya ulinzi"

Psalms 38

Psalms 38:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

usinikemee katika hasira yako ... usiniadhibu katika gadhabu yako

Misemo hii inamaana moja na wazo linarudiwa kwa ajili ya mkazo.

mishale yako inanichoma

Ukali wa adhabu ya Yahwe kwa mwandishi unazungumziwa kana kwamba Yahwe amepiga mishale kwa mwandishi. "Adhabu yako ina maumivu kana kwamba umepiga mishale kwangu"

mkono wako unanikandamiza chini

Adhabu ya Yahwe kwa mwandishi inazungumziwa kana kwamba Yahwe alikuwa akimponda mwandishi kwa mkono wake.

Psalms 38:3

Taarifa ya Jumla:

Daudi anaendelea kueleza kile amabacho hatia na aibu yake inavyoufanya mwili wake. Anatumia kauli iliyokuzwa kuweka mkazo madhara ya somo hili.

hakuna afya katika mifupa yangu kwa sababu ya dhambi yangu

Hapa "mifupa yangu" inawakilisha mwili wa mwandishi. "mwili wangu wote unaugonjwa kwa sababu ya dhambi yangu"

udhalimu wangu unanilemea

Udhalimu wa mwandishi unazungumziwa kana kwamba ni mafuriko ya maji yanayomfunika. "udhalimu wangu unanifunika kama mafuriko"

ni mzigo mzito sana kwangu

Udhalimu wa mwandishi unazungumziwa kana kwamba ni mzigo asioweza kuinua. "ni kama mzigo ulio mzito sana kwangu kunyanyua"

Psalms 38:5

Taarifa ya Jumla:

Daudi anaendelea kueleza kile amabacho hatia na aibu yake inavyoufanya mwili wake. Anatumia kauli iliyokuzwa kuweka mkazo madhara ya somo hili.

Vidonda vyangu vimeathirika na vinanuka

Hapa "kunuka" inamaanisha vidonda vyake kuwa na harufu mbaya inayoambatana na kuoza kwa nyama. "Vidonda vyangu vimeathirika na vinanuka vinavyooza"

Nimeinama

Maumivu ya mwandishi yamemsababisha ainame kana kwamba ni mzee aliyechoka. "Nimeinama kwa maumivu"

Psalms 38:7

nimejawa na kuungua

Mwandishi ana homa sana hadi inakuwa kana kwamba anaungua ndani. "Mwili wangu unachemka kwa homa"

hakuna afya katika mwili wangu

Hapa "mwili" unamaanisha mwandishi. "Ninaumwa sana"

kupondeka kabisa

Ugonjwa wa mwandishi ni mkali sana hadi inakuwa kana kwamba uzito unamkandamiza chini.

uchungu wa moyo wangu

Hapa "moyo wangu" unamaanisha mwandishi. "uchungu wangu"

Psalms 38:9

haja zangu za moyo za ndani

Hapa "moyo" unamaanisha mwandishi. "Hamu zangu kuu" au "kuwa natamani uniponye"

magumio yangu hayajafichwa kwako

Hii inaweza kuelzwa katika hali ya kutenda. "unaweza kuona

moyo wangu unadunda

"unaweza kuona kulia kwangu kwa huzuni"

nguvu yangu inapotea

"ninakuwa mnyonge sana"

kuona kwangu kunafifia

"Siwezi kuona vizuri tena"

Psalms 38:11

wanalaza mitego kwa ajili yangu

Mipango ya waandishi wa adui wanazungumziwa kana kwamba ni mitego walitega kumshika kama mnyama. "kuweka mitego kunishika"

huzungumza maneno ya uharibifu na kusema maneno ya udanganyifu

Misemo hii miwili inamaanisha kitu kimoja na inasisitiza uasili wa kuumiza wa kile ambacho watu hawa wanasema.

Psalms 38:13

Niko kama kiziwi ... sisikii ... asiyesikia

Mistari ya kwanza ya mstari wa 13 na 14 inatumia tashbihi kuwakilisha picha moja ya mtu kiziwi. Mwandishi anaumwa sana hadi hasikii.

Mimi ni kama bubu ... hasemi kitu ... hana jibu

Mistari ya kwanza ya mstari wa 13 na 14 inatumia tashbihi kuwakilisha picha moja ya mtu bubu. Mwandishi anaumwa sana hadi hazungumzi.

bubu

mtu asiyeweza kuongea

Psalms 38:15

utajibu

Maana zinazowezekana ni 1) "utanijibu" au 2) "utawajibu adui zangu."

wasinicheke

"hawatafurahi juu ya shida yangu"

Kama mguu wangu ukiteleza

Hapa "mguu" unmwakilisha mwandishi. Kuteleza kwa mguu wake ni sitiari inayomaanisha matatizo ya mwandishi na bahati mbaya. "Kama nikifanya makosa ya kunisababishia taabu"

Psalms 38:17

ninataka kujikwaa

Maana zinazowezekan kwa sitiari hii ni 1) "ninaumwa sana hadi ninataka kufa" au 2) "nitaangamia hivi karibuni."

niko kwenye maumivu endelevu

"niko kwenye maumivu daima"

Psalms 38:19

Lakin adui wangu ni wengi ... ni wengi

Misemo hii miwili inamaana sawa.

Wananilipa uovu kwa uzuri

Matendo ya adui wa mwandishi yanazungumziwa kama mapatano ya kibiashara ambapo walimpa vitu viovu kwa kubadilishana na vitu vizuri. "Wananipa matendo maovu kwa kubadilishana na matendo yangu mazuri kwao"

wanatupa mashtaka kwangu

Jinsi adui wa mwandishi wanavyomshtaki inazungumziwa kana kwamba wanatupa mashtaka kwake kama mawe.

nimefuata kilicho chema

Hamu ya mwandishi kwa kilicho chema kinazungumziwa kana kwamba anakimbilia vitu vizuri.

Psalms 38:21

Usiniache ... usikae mbali na mimi

Misemo hii miwili ina maana za kufanana sana.

usikae mbali na mimi

Kwa sababu Yahwe bado hajajibu ombi la mwandishi, anamzungumzia Yahwe kana kwamba yahwe alikuwa amesimama mbali na mwandishi.

Njoo upesi kunisaidia

Mungu anazungumziwa kana kwamba anakimbia kwenda kwa mwandishi kumsaidia.

wokovu wangu

"wewe ndiye unayeniokoa"

Psalms 39

Psalms 39:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Yeduthuni

Mmoja wa wanamuziki wakuu wa Daudi alikuwa na jina hili. Hii inaweza kumaanisha ni yeye.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Nitachunga ninachozungumza

"Nitakuwa msikivu katika vitu nitakavyosema"

ili nisitende dhambi kwa ulimi wangu

Hapa "ulimi" inamaanisha maneno ya mwandishi. "ili nisizungumze maneno mabaya dhidi ya Yahwe"

nitajitia lijamu

Hii inamaanisha kufunga mdomo. Hapa Daudi anamaanisha kuwa hatazungumza akiwa na mtu mwovu.

Psalms 39:2

Nilikaa kimya; nilitunza maneno yangu

Misemo hii miwili inamaana moja na inasisitiza kuwa mwandishi hakuzungumza kabisa. "Nilikuwa kimya kabisa"

nilitunza maneno yangu

Hapa "maneno yangu" inamaanisha maneno ya mwandishi. "sikuzungumza"

Moyo wangu ukachemka ... ukawaka kama moto

Hapa "moyo" unamwakilishi mtu mzima. Mawazo ya wasiwasi ya mwandishi yanazungumziwa kana kwamba ni moto unaomuunguza ndani yake. "Nikawa na wasiwasi sana nilipowaza hivi vitu"

Psalms 39:4

mwisho wa maisha yangu ... kiasi cha siku zangu

Misemo hii inamaana moja.

Nioneshe jinsi nilivyo wa kupita

"Nioneshe jinsi maisha yangu yalivyo mafupi" au "Nioneshe nitakavyokufa mapema"

upana wa mkono wangu tu

Mwandishi anazungumza kana kwamba yanaweza kupimwa na upana wa mkono wake. "muda mdogo sana"

maisha yangu ni kama bure mbele yako

Tashbihi hii inaeleza kuwa urefu wa maisha ya mwandishi ni mafupi sana hadi hayapo. Hii ni kukuza kwa neno kuonesha jinsi yalivyo mafupi. "urefu wa maisha ni muda kidogo sana"

Hakika kila mtu ni pumzi moja

Ufupi wa maisha unazungumziwa kana kwamba ulikuwa ni sawa na muda unaochukua mtu kupumua mara moja. "Muda ambao wanadamu huishi ni mfupi kama pumzi moja ya mtu"

Psalms 39:6

Hakika kila mtu anatembea kama kivuli

Maisha ya watu yanazungumziwa kana kwamba sio ya muhimu kama vivuli. "Kila mtu anapotea kama vivuli vinavyofanya"

ingawa hawajui nini atawapokea

Hapa inadokezwa kuwa hawajui kitakachotokea kwa utajiri watakapokufa.

Sasa, Bwana, ninasubiri nini?

Mwandishi anauliza hili swali kusisitiza kuwa watu hawawezi kumsaidia. "Kwa hiyo, Yahwe, sitegemei kupokea kitu kutoka kwa mtu mwingine"

Psalms 39:8

Niko kimya ... siwezi kufungua mdomo wangu

Misemo hii inamaana moja.

kwa sababu ni wewe uliyekifanya

""kwa sababu adhabu yangu inatoka kwako"

Psalms 39:10

Acha kuniumiza

Adhabu ya Mungu kwa mwandishi inazungumziwa kana kwamba Mungu alikuwa akimuumiza kwa silaha. "tafadhali acha kuniadhibu!"

nimelemewa

"nimeshindwa kabisa"

pigo la mkono wako

Adhabu ya Mungu kwa mwandishi inazungumziwa kana kwamba Mungu alikuwa akimpiga kwa mkono wake. Hapa "mkono" unawakilisha hukumu ya Mungu. "hukumu yako kwangu"

unameza vitu wanavyotamani kama nondo

Mungu atachukua vitu wanavyojali katika njia moja nondo anavyokula kipande cha nguo. "unameza vitu wanavyotamani kama nondo anavyokula nguo"

watu wote sio kitu ila mvuke

Mwandishi anazungumza udhaifu wa watukana kwamba ni umande unaopotea haraka. "kila mtu ni dhaifu kabisa"

Psalms 39:12

Sikia ombi langu ... nisikilize ... sikia kilio changu

Misemo hii mitatu inamaana moja na inaonesha jinsi mwandishi anavyotaka Mungu amjibu.

Usiwe kiziwi kwangu

Mwandishi anazungumzia Yahwe kutomjibu kana kwamba ni kiziwi. "Usiache kunijali kana kwamba huwezi kunisikia"

Mimi ni kama mgeni kwako, mkimbizi

Mwandishi anazungumzia Yahwe kutomjibu kana kwamba Yahwe alikuwa akimchukulia kama mgeni kabisa kwake. "Mimi ni kama mgeni kabisa kwako"

Usinikazie macho

Hapa "kukazia macho" inawakilisha adhabu ya Yahwe. "Tafadhali acha kuniadhibu"

ili ni tabasamu tena

Hapa "kutabasamu" inahusishwa na kuwa na furaha. "ili niweze kuwa na furaha tena"

Psalms 40

Psalms 40:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Nilimsubiri Yahwe kwa uvumilivu

Hii inamaanisha mwandishi alimsubiri Yahwe kumsaidia.

alinisikiliza ... kusikia kilio changu

"alinisikia nilipomwita"

nje ya shimo baya, nje ya udongo wa tope

Sitiari hizi mbili zinamaanisha kitu kimoja. Hatari ya mwandishi inazungumziwa kana kwambani shimo hatari la tope. Hii inawekea mkazo hatari. "kutoka kunaswa kwenye shimo baya lililojaa tope ya kunata.

ameweka miguu yangu kwenye mwamba

Hapa "miguu" inamaanisha ni mwandishi, na "mwamba" inamaanisha sehemu ya usalama. "alitoa usalama kwa ajili yangu"

Psalms 40:3

Ameweka wimbo mpya mdomoni mwangu

Maana zinazowezekana ni 1) "Amenifundisha maneno ya wimbo mpya" au 2) "Amenipa sababu mpya ya kuimba"

mdomoni mwangu

Hapa "mdomo wangu" inamaanisha mwandishi. "ndani yangu"

sifa kwa Mungu wetu

"wimbo wa kumsifu Mungu wetu"

Wengi wataona

Hapa "wataona" inamaanisha kumsikia mwandishi akiimba wimbo kuhusu kile ambacho Mungu amemtendea. "Watu wengi watasikia kile ambacho Yahwe amefanya"

Amebarikiwa mtu anayemfanya Yahwe tumaini lake

"Amebarikiwa mtu anayemtumaini Yahwe" au "Wale wanaomtumaini Yahwe wamebarikiwa"

wenye kiburi

Hii inamaanisha watu walio na kiburi.

uongo

Maana zinazowezekana ni 1) "uongo" au 2) "miungu ya uongo"

Psalms 40:5

Mawazo yako juu yetu hayahesabiki

"hakuna mtu awezaye kuhesabu vitu vyote unavyotuwazia"

hayahesabiki ... zaidi ya yanayoweza kuhesabika

Misemo hii inamaana sawa. Ya kwanza imeelezwa katika hali hasi na ya pili katika hali chanya.

Haupendezwi na dhabihu na sadaka

Hii ni kukuza kwa neno ili kuonesha kuwa vitu hivi havikuwa muhimu zaidi kwa Mungu. "Dhabihu na sadaka zingine sio vitu vinavyokufurahisha zaidi"

umefungua maskio yangu

Hapa "maskio" inamaanisha uwezo wa kusikia. "umeniwezesha kusikia amri zako"

hujaomba sadaka za kuchoma au sadaka za dhambi

Hii ni kukuza kwa neno ili kuonesha kuwa vitu hivi havikuwa muhimu zaidi kwa Mungu. "wanyama wanaotolewa kwenye madhabahu na sadaka zingine kwa ajili ya dhambi zetu sio unachotaka zaidi"

Psalms 40:7

gombo la nyaraka

Hii inamaanisha gombo ambapo kuna neno la kuandikwa la Yahwe. "gombo lililoandikwa"

sheria zako ziko moyoni mwangu

Hapa "moyo" inamaanisha undani wa mwanshishi. "Huwa ninawaza kuhusu sheria zako ndani mwangu"

Nimetangaza habari njema za haki yako katika mkusanyiko mkuu

"Nimewaambia mkusanyiko mkubwa wa watu habari njema za haki yako"

habari njema za haki yako

Hii inamaanisha habari njema kuwa Mungu huokoa watu wake. "habari njema kwa sababu u mwenyehaki, unaokoa watu wako"

midomo yangu yaijajizuia kufanya hili

Hapa "midomo" inamaanisha maneno ya mwandishi. "Sijajizuia kutangaza hivi vitu"

Psalms 40:10

Sijaficha haki yako moyoni mwangu

"Sijafanya haki yako kuwa siri" au "Nimemweleza kila mtu kuhusu haki yako"

moyoni mwangu

Hapa inamaanisha hali ya ndani.

Sijaficha uaminifu wako wa agano au uaminifu wako kwenye mkusanyiko mkuu

"Nimemwambia watu wote katika kusanyiko kuu kuhusu uaminifu wako wa agano au uaminifu wako"

uaminifu wako wa agano

"jinsi ulivyo mwaminifu kutunza ahadi zako"

uaminifu wako

"jinsi ulivyo mwaminifu"

acha uaminifu wako wa agano na uaminifu wako unitunze

Hapa "uaminifu wa agano" na "uaminifu" zinazungumziwa kana kwamba ni binadamu hai wanaoweza kumlinda mwandishi. "nataka uaminifu wako wa agano na uaminifu wako unilinde daima"

Psalms 40:12

Taabu zisizoweza kuhesabika zinanizunguka

Hapa taabu zinazungumziwa kana kwamba ni vitu vinavyomzunguka na kumtega mwandishi. "kuna taabu nyingi zimenizunguka kuliko navyoweza kuhesabu" au "taabu nyingi huja kwangu kuliko navyoweza kuhesabu"

zisizoweza kuhesabika

Hii imeelezwa katika hali hasi kuweka mkazo wa idadi. "zilizo nyingi kwa idadi"

udhalimu wangu

Hii inamaanisha matokeo ya dhambi. "matokeo ya udhalimu wangu"

umenishika

Udhalimu wa mwandishi unazungumziwa kana kwamba ni adui zake wanaomdhuru.

siwezi tena kuona kitu

Matoleo yanatofautiana katika kuelewa msemo huu. Inaweza kuwa inamaanisha kuwa mwandishi analia sana hadi hawezi kuona chochote kwa sababu ya machozi yake.

moyo wangu umeshinda

Hapa "moyo" inamaanisha ujasiri wa ndani wa mwandishi.

Psalms 40:14

Acha ... wanaofuatilia maisha yangu kuyachukua

"Tafadhali wafanye wale wanaojaribu kuniua waaibike na kuvunjwa matumaini"

wanaofuatilia maisha yangu kuyachukua

Hapa "wanaofuatilia maisha yangu" inamaanisha hamu ya kumuua mwandishi. "wanaojaribu kuniua"

Acha ... wanaofurahi kuniumiza

"Tafadhali wasimamishe wale wanaofurahi kuniumiza na uwatolea heshima"

wageuzwe

Kuzuiliwa inazungumziwa kama kugeuzwa kutoka katika mashambulizi yao. "kuzuiwa"

Acha ... wanaosema, "Aha, aha!"

"Acha wale wanaosema kwangu, 'Aha, aha!' washtuke kwa sababu ya aibu yao"

Acha washtuke kwa sababu ya aibu yao

"Natamani washtuke utakapowaaibisha"

wale wanaosema kwangu, "Aha, aha!"

"Aha, aha!" ni kitu wanachosema watu wakati wakimdhihaki mtu.

Psalms 40:16

washangilie na kuwa na furaha

Misemo hii miwili inamaanisha kitu kimoja na inasisitiza uzito wa furaha. "wawe na furaha sana"

wanaopenda wokovu wako

"wanaokupenda kwa sababu umewaokoa"

maskini na mhitaji

Maneno haya yanamaanisha kitu kimoja na yanasisitiza jisni mwandishi asivyojiweza. "mhitaji sana"

Bwana ananiwaza

"Bwana ananijali"

Wewe ni msaada wangu ... unakuja kwa ukombozi wangu

Misemo hii inamaanisha kitu kimoja.

Wewe ni msaada wangu

"Wewe ndiye unaye nisaidia"

unakuja kwa ukombozi wangu

"unakuja kunioka"

usichelewe

"unijibu upesi"

Psalms 41

Psalms 41:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

yeye ... atamwokoa ... zake

Anayezungumziwa hapa ni mtu anayejihusisha na wanyonge.

wanyonge

"watu wanyonge" au "watu maskini"

Yahwe atamsaidia katika kitanda cha mateso

Msemo "kitanda cha mateso" inamaanisha mtu anapolala kitandani kwa sababu ni mgonjwa. "Akiwa mgonjwa na kitandani, Yahwe atamlinda"

utakifanya kitanda cha magonjwa yake kuwa kitanda cha uponyaji

Msemo "kitanda cha uponyaji" inamaanisha mtu anapopumzika kitandani na kupona ugonjwa wake. "wewe, Yahwe, utamponya ugonjwa wake"

Psalms 41:4

jina lake lipotee

Kama jina la mtu linakufa, inamaanisha kuwa watu wanasahau kuwa aliwahi kuishi. "jina lake litapotea lini" au "watu watasahau lini jina lake"

Kama adui wangu akija kuniona

Maneno "adui wangu" inamaanisha adui yeyote kwa ujumla, na sio kwa adui bayana yeyoto.

anasema vitu visivyofaa

Maana zinazowezekana ni 1) "anasema vitu vya kipuuzi" au 2) adui zake wanasema vitu kumfanya afikiri kuwa ni rafiki zake wakati sio. "anasema vitu vya udanganyifu" au "wanajifanya kumjali"

moyo wake unajikusanyia wenyewe maafa yangu

Adui zake wanajaribu kujifunza vitu vyote vibaya kumhusu. Hapa neno "moyo" linamaanisha mtu mzima. Matukio mabaya yanazungumziwa kana kwamba ni vitu vinavyoweza kukusanywa. "anajaribu kujifunza kuhusu maafa yangu yote"

Psalms 41:7

wanatamani niumie

Maana zinazowezekana ni 1) "wanatamani kwamba vitu vibaya sana vinikute" au 2) "wanapanga kunidhuru"

Ugonjwa uovu ... kwake

Adui zangu wanazungumzia "ugonjwa" kana kwamba ni mtu aliyemkamata. "Ni mgonjwa na ugonjwa hatari"

Ugonjwa uovu

Maana zinazowezekana ni 1) "ugonjwa wa mauti" au 2) "Kitu kiovu"

kwa sasa amelala chini, hatainuka tena

Hapa maneno "amelala chini" inamaanisha kulala kitndani kwa sabau ya ugonjwa. Kuwa "hatainuka" inamaanisha ataendelea kulala chini, ambayo pia tasifida ya kifo. "kwa kuwa sasa yuko kitandani, atakufa hapo"

ameinua kisigo chake dhidi yangu

Hii ni lahaja inayomaanisha rafiki yake amemsaliti. "amenisaliti" au "amegeuka dhidi yangu"

Psalms 41:10

Lakini wewe, Yahwe, unahuruma kwangu na unaniinua

Hili ni ombi. "Tafadhali, Yahwe, uwe na huruma kwangu na niinue"

unaniinua

Hii inamaanisha kumwinua kutoka kitandani, au kumponya kutoka kwenye ugonjwa wake.

ili niweze kuwalipa

Mwandishi anazungumzia kisasi kwa adui zake kana kwamba ni kuwalipa anachodaiwa. "ili kwamba nilipe kisasi kwao"

Kwa hili najua kuwa unafurahishwa na mimi, kwa kuwa adui wangu hanishindi

Neno "hili" inamaanisha kile ambacho mwandishi atasema baadaye. "Kwa sababu adui wangu hanishindi, natambua kuwa unafurahishwa na mimi"

Kwa hili najua kuwa unafurahishwa na mimi, kwa kuwa adui wangu hanishindi

"Ukiniwezesha kutenda hilo, kwa matokeo ya adui zangu kushindwa kunishinda, nitajua kuwa umefurahishwa na mimi"

unanibeba katika uadilifu wangu

"unanilinda kwa sababu ya uadilifu wangu"

utaniweka mbele ya uso wako

Mwandishi anazungumzia kuwa katika uwepo wa Yahwe kama kuwa sehemu ambayo Yahwe anaweza kumuona na kuona uso wa Yahwe. "utaniweka pamoja na wewe"

Psalms 41:13

Taarifa ya Jumla:

Mstari huu ni zaidi ya mwisho wa zaburi hii. Ni kauli ya kufunga ya kiabu chote cha kwanza cha Zaburi, kinachoanzia katika Zaburi 1 na kuishia na Zaburi 41.

kutoka milele na milele

Hii inamaanisha tofauti mbili na inamaanishwa wakati wote. "milele"

Amina na Amina

Neno "Amina" linarudiwa kusisitiza kukubaliwa kwa kilichosemwa. "Na hakika iwe hivyo"

Psalms 42

Psalms 42:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Maschili

Hii inaweza kumaanisha mtindo wa muziki.

Kama mbawala anavyotweta kwa ajili ya kijito cha maji, vivyo hivyo ninakiua na wewe , Mungu

Mwandishi analinganisha shauku yake kwa ajili ya Mungu na shauku ya mbawala kwa ajili ya maji.

anavyotweta

kupumua kwa nguvu kutoka kwa mnyama au mtu aliyechoka sana au mwenye kiu

ninakiua na wewe , Mungu ... Ninakiu na Mungu

Mwandishi anazungumzia hamu yake kubwa kwa ajili ya Mungu kana kwamba ni kiu kikali kwa ajili ya maji.

nitakuja lini nakutokea mbele za Mungu?

Mwandishi haulizi swali hili ili kupata jibu bali kuonesha shauku yake kubwa ya kuwa mbele za Mungu.

Psalms 42:3

Machozi yangu yamekuwa chakula changu

Mwandishi anazungumzia machozi yake kana kwamba ni chakula anachokula. Hii inamaanisha kuwa ana huzuni sana hadi hawezi kula. "Machozi yangu ni kama chakula changu na sili kitu kingine"

mchana na usiku

Msemo huu unamaanisha siku nzima kwa kutaja mwanzo wake na mwisho wake. "siku nzima"

adui zangu daima wanasema kwangu

Huku ni kukuza kwa neno. Adui zake hawasemi haya muda wote; wanasema mara kwa mara.

Yuko wapi Mungu wako?

Adui wa mwandishi wanatumia swali hili kumkejeli na kuonesha kuwa hawaoni Mungu wake akimsaidia. "Mungu wako hayuko hapa kukusaidia"

itisha akilini

Hii ni lahaja inayomaanisha kuwaza au kukumbuka kitu. "kumbuka"

Ninamwaga nafsi yangu

Hapa neno "nafsi" inamaanisha hisia. Mwandishi anazungumzia nafsi yake kana kwamba ni kimiminiko anachomwaga. Msemo unamaanisha kuwa anaeleza uchungu wake wa hisia. "ninaeleza huzuni yangu"

msongamano

"kundi la watu"

furaha na sifa

Msemo huu unatumia maneno mawili tofauti kueleza wazo moja.

Psalms 42:5

Kwa nini umeinama chini, nafsi yangu? Kwa nini umefadhaika ndani yangu?

Mwandishi jizungumzia undani wake kama "nafsi" yake. Anajiuliza maswali haya kujikemea. "Sitakiwi kuinama chini. Sitakiwa kuwa na wasiwasi"

umeinama chini

Mwandishi anazungumzia huzuni au kukata tamaa kana kwamba nafsi yake imeinama. "kukata tamaa"

Mtumaini Mungu

Mwandishi anaendelea kuzungumza na nafsi yake na kuiamuru kumtumaini Mungu.

Mungu wangu, nafsi yangu

Mwandishi anaanza kuzungumza na Mungu kuhusu nafsi yake.

Nina kuiitisha akilini

Msemo huu unamaanisha kukumbuka au kuwaza kuhusu kitu. "Nina kuwaza"

nchi ya Yordani

Hii inaweza kumaanisha Israeli ya kaskazini, ambapo mto Yordani huanzia. "nchi ambayo mto Yordani huanzia"

vilele

juu ya milima

kilima cha Mizari

Hili ni jina la kilima kwenye kitako cha mlima Hermoni.

Psalms 42:7

Kilindi huita kilindi katika kelele cha maporomoko

Neno "kilindi" inmaanisha maji yenye kina kirefu, ambapo hapa inawezekana ni vijito vinavyo tiririka chini ya mlima Hermoni. Mwandishi anavizungumzia kana kwamba ni watu wanaitana wanaposikia sauti yao ya kushuka katika mlima.

mawimbi yako yote ... yameenda juu yangu

Mwandishi anazungumzia bahati yake mbaya na huzuni kana kwamba ni maji yenye kina kirefu yanayo mzamisha kwa wimbi moja baada ya jingine.

mawimbi yako na gharika

Maneno haya mawili yanatumika pamoja kusisitiza ukubwa wa mawimbi. "mawimbi yako yote makubwa"

Yahwe ataamuru uaminifu wake wa agano

Mwandishi anazungumzia uaminifu wa agano wa Yahwe kana kwamba ni mtu anayemwamuru kuwa naye. "Yahwe atanionesha uaminifu wake wa agano"

wimbo wake

Maana zinazowezekana ni 1) "wimbo anaonipa" au "wimbo kumhusu"

Mungu wa uhai wangu

"Mungu anayenipa uhai"

Psalms 42:9

Nitasema kwa Mungu, mwamba wangu

Mwandishi anamzungumzia Mungu kana kwamba ni mwamba mkubwa utakaotoa ulinzi dhidi ya mashambulizi ya adui.

Kwa nini ninaenda kuomboleza

"Kwenda kuomboleza" nikufanya desturi zinazokaribiana na kuwa huzuni sana.

Kama na upanga ndani ya mifupa yangu

Mwandishi anaelezea kukemea kwa adui zake kama kupokea kidondo hatari.

huwa wanasema kwangu

Hii ni ukuzaji wa neno; adui zake hawasemi hivi kila wakati bali wanasema mara kwa mara.

Yuko wapi Mungu wako?

Adui wa mwandishi wanatumia swali hili kumkejeli na kuonesha kuwa hawaoni Mungu wake akimsaidia. "Mungu wako hayuko hapa kukusaidia"

Psalms 42:11

Kwa nini umeinama chini, nafsi yangu? Kwa nini umefadhaishwa ndani yangu?

Mwandishi jizungumzia undani wake kama "nafsi" yake. Anajiuliza maswali haya kujikemea. "Sitakiwi kuinama chini. Sitakiwa kuwa na wasiwasi"

umeinama chini

Mwandishi anazungumzia huzuni au kukata tamaa kana kwamba nafsi yake imeinama. "kukata tamaa"

Mtumaini Mungu

Mwandishi anaendelea kuzungumza na nafsi yake na kuiamuru kumtumaini Mungu.

Psalms 43

Psalms 43:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Mungu wa nguvu yangu

Maana zinazowezekana ni 1) "Mungu unayenilinda" au 2) "Mungu unayenipa nguvu"

Kwa nini umenikataa? Kwa nini ninaomboleza kwa sababu ya ukandamizaji wa adui?

Mwandishi anauliza maswali haya ili kulalamika kwa Mungu na kuonesha hisia yake, sio kupata jibu.

Kwa nini ninaomboleza

"Kuomboleza" ni kufanya matendo yana onesha kuwa na huzuni sana.

kwa sababu ya ukandamizaji wa adui

Neno "ukandamizaji" linaweza kutafsiriwa kama kitenzi. "kwa sababu adui zangu wananikandamiza"

Psalms 43:3

tuma nuru yako na ukweli wako

Mwandishi anazungumzia ukombozi wa Mungu kana kwamba ni nuru inayo mwonyesha njia na ukweli unaomfundisha jinsi ya kuishi. "niongoze kwa nuru yako na kweli"

mlima ... mtakatifu

Hii inamaanisha mlima ulioko Yerusalemu ambapo hekalu lipo kwa hiyo ni hekalu lenyewe.

kwenye makazi yako

"mahali ambapo unaishi"

Mungu furaha yangu inayozidi

"Mungu ambaye ni furaha yangu kubwa sana" au "Mungu anayenipa furaha kubwa"

Psalms 43:5

Kwa nini umeinama chini , nafsi yangu? Kwa nini umekasirika ndani yangu?

Mwandishi anaelezea uwepo wake wa ndani kama "nafsi" yake. Anauliza maswali haya kujikemea mwenyewe. "Sitakiwi kuinama chini. Sitakiwi kuwa na wasiwasi"

umeinama chini

Mwandishi anazungumzia huzuni au kukata tamaa kana kwamba nafsi yake imeinama.

Mtumaini Mungu

Mwandishi anaendelea kuzungumza na nafsi yake na kuiamuru kumtumaini Mungu.

wokovu wangu na Mungu wangu

Msemo "wokovu wangu" inamaanisha Mungu. Ikibidi, misemo miwili inaweza kuunganishwa. "Mungu wangu anayeniokoa"

Psalms 44

Psalms 44:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kihebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Zaburi ya wana wa Kora

"Hii ni zaburi ambayo wana wa Kora waliandika."

Maschili

Hii inaweza kuwa mtindo wa muziki.

Tumeskia kwa maskio yetu, Mungu

Neno "maskio" linaongeza mkazo kwa kauli waliosikia na kuelewa vitu ambavyo mwandishi anataka kueleza. Mwandishi anaeleza kauli hii kwa Mungu. "Mungu, tumesikia vizuri"

katika siku zao, katika siku za kale

Misemo yote hii miwili inatumia neno "siku" kumaanisha wakati ambao mababu wa watu wa Israeli walipokuwa hai.

Uliondoa mataifa

"Ulilazimisha watu wa mataifa mengine kuondoka"

kwa mkono wako

Hapa neno "mkono" linamaanisha nguvu ya Mungu. "kwa nguvu yako"

uliwapanda watu wetu

Mwandishi anamzungumzia Mungu kusababisha Waisraeli kuishi katika nchi kana kwamba aliyokuwa akiwapanda katika udongo kama ambavyo angepanda mti. "uliwasababisha watu kuishi huko"

Psalms 44:3

kwa upanga wao wenyewe

Neno "upanga" linamaanisha nguvu ya kijeshi. "kwa kupigana na panga zao" au "kwa nguvu ya jeshi lao wenyewe"

mkono wao wenyewe

Hapa neno "mkono" linamaanisha nguvu. "nguvu yao wenyewe"

na nuru ya uso wako

"na nuru ya uso wako uliwapatia nchi kuwa mali yao"

mkono wako wa kuume, mkono wako

Hapa neno "mkono" linamaanisha nguvu ya Mungu. Kwa pamoja zinaweka mkazo kwa ukuu wa nguvu ya Mungu. "nguvu yako kuu"

nuru ya uso wako

Mwandishi anamzungumzia Yahwe kuwaangalia kwa fadhila na kuwa na huruma kwao kana kwamba ni uso wa Yahwe ulitoa nuru kwa ajili yao. "huruma yako" au "fadhila zako"

ushindi kwa Yakobo

Watu wa Israeli wanajulikana kwa jina la babu yao "Yakobo"

Psalms 44:5

Kupitia kwako ... kupitia

"Kwako ... kwa"

tutasukuma ... kuwakanyaga chini ... inuka juu

Mwandishi anazungumzia kushindwa kwa adui zake kana kwamba wako "chini" na kujiandaa kwao kupigana kana kwamba wako "juu."

kupitia jina lako

Hapa neno "jina" linamaanisha nguvu na mamlaka ya Mungu. "kwa nguvu yako"

kuwakanyaga chini

"kuwakanyaga chini ya miguu yako" au "kutembea juu yao"

Psalms 44:7

tumefanya majivuno yetu

"tumejivuna"

tutatoa shukrani kwa jina lako

Hapa neno "jina" linamaanisha Mungu mwenyewe. "tutakupa shukrani wewe"

Psalms 44:9

umetutupa

Mwandishi anazungumzia kukataliwa kwa Israeli kana kwamba alikuwa akitupa nguo ambayo haitaki. "kutukataa"

ngawira

mali ambazo jeshi hukusanya baada ya kushinda vita

Umetufanya kama kondoo waliokusudiwa kuwa chakula

Mwandishi anafananisha Waisraeli na kondoo ambao watu huua na kula. Kama kondoo wasiojiweza mbele ya wale wanaowaua, kwa hiyo Waisraeli hawajiwezi mbele ya adui zao. "Umewaruhusu adui zetu kutuua kama wanavyoua kondoo na kumla"

waliokusudiwa kuwa chakula

"tumekusudiwa kuwa chakula ambacho watu wanakula"

kututawanya miongoni mwamataifa

"kutusababisha kuishi katika mataifa mengi tofauti"

Psalms 44:12

Unawauza watu wako bure

Mwandishi anamzungumzia Yahwe kuwaruhusu adui wa Israeli kuwashinda kana kwamba alikuwa akiwauza watu wa Israeli kwa adui zao lakini hahitaji malipo kutoka kwa adui zao.

Unatufanya kuwa lawama kwa jirani zetu, kudhihakiwa na kukejeliwa na wale waliotuzunguka

Misemo hii miwili ina usambamba ikisisitiza jinsi watu wanaoishi miongoni mwao wanavyowakejeli.

Unatufanya kuwa lawama kwa jirani zetu

"Unatufanya kuwa kitu ambacho jirani zetu wanakemea"

kudhihakiwa na kukejeliwa na wale waliotuzunguka

"wale waliotuzunguka wanatudhihaki na kutukejeli"

fedheha miongoni ... kutikisa kichwa

Misemo hii miwili ina usambamba ikisisitiza jinsi watu wanavyowakejeli kwa nguvu.

Umetufanya fedheha miongoni mwa mataifa

Unayafanya mataifa yaliyo tuzunguka kutufedhehesha"

kutikisa kichwa miongoni mwa watu

"jambo ambalo watu hutikisa vichwa"

kutikisa kichwa

Hiki ni kitendeo ambacho watu walitumia kuonesha dharau wengine.

Psalms 44:15

fedheha yangu iko mbele yangu

Mwandishi anazungumzia fedheha kana kwamba ni kitu ambacho daima kiko mbele yake kwa ajili yake kuona. Msemo unamaanisha kuwa huwa anafikiria fedheha yake. "ninafikiria fedheha yangu"

aibu ya uso wangu umenifunika

Mwandishi anazungumzia aibu yake kana kwamba ni kitu kinachomfunika kama blangeti. "aibu ya uso wangu imenilemea"

aibu ya uso wangu

"aibu inayoonekana katika uso wangu." Hii inamaanisha mwonekano wa sura ambao unasababishwa na aibu yake.

kwa sababu ya sauti ya yule anyenikemea na kunifedhehesha

Hapa neno "sauti"linamaanisha kitu ambacho mtu anasema. "kwa sababu ya kile ambacho mtu anasema anyenikemea na kunifedhehesha"

anyenikemea na kunifedhehesha

Maneno haya yana maaza za kufanana na yanasisitiza uhalisia mbaya wa kile ambacho mtu huyu anasema.

Psalms 44:18

Moyo wetu haujageuka ... hazijatoka kwenye njia yako

Misemo hii miwili in usambamba. Mwandishi anazungumzia uaminifu kwa Mungu kana kwamba ilikuwa kumfuata, na kutokuwa mwaminifu kana kwamba ni kumgeuka.

Moyo wetu haujageuka

Hapa neno "moyo" linamaanisha hisia, hasa za uaminifu. "Hatujaacha kuwa waaminifu kwako"

umetuvunja sana

Mwandishi anazungumzia adhabu za Mungu kana kwamba ilikuwa ni kuvunja chombo rahisi kuvunjika. "umetuadhibu vikali"

katika nafasi ya mbweha

Mwandishi anazungumzia Israeli baada ya adhabu ya Mungu kana kwamba ilikuwa sehemu ya pori, ambapo mtu hawezi kuishi. "umefanya nchi yetu kama sehemu ambayo mbweha huishi"

mbweha

aina ya mbwa pori

kutufunika na kivuli cha mauti

Mwandishi anazungumzia mauti kana kwamba ni kitu kinachotoa kivuli juu ya wale wanaotaka kufa. "umetufanya ili tuwe karibu kufa"

Kama tumesahau jina la Mungu wetu

Hapa neno "jina" linamaanisha Mungu mwenyewe. Kumsahau Mungu ni kuacha kumwabudu. Hili ni jambo ambalo halikutokea. "Kama tungemsahau Mungu wetu" au "Kama tungeacha kumwabudu Mungu wetu"

kusambaza mikono yetu kwa mungu mgeni

Kusambaza mikono ni ishara ambayo watu walitumia kuabudu na kuomba kwa mungu yeyote. "waliabudu mungu mgeni" au "kuomba kwa mungu mgeni"

Je, Mungu hatalichunguza hili?

Mwandishi anatumia swali hili kueleza kuwa Mungu atajua kama watamwabudu mungu mwingine. "Hakika Mungu atagundua"

anajua siri zatunauwawa siku nzima moyo

Hapa neno "moyo" unamaanisha akili na mawazo. "anajua kile ambacho mtu anawaza kwa siri"

tunauwawa siku kutwa

Msemo "siku kutwa" ni kukuza maneno kusisitiza kuwa watu wao wanauwawa mara kwa mara. "watu wanatuua kila wakati"

tumefanywa kuwa kondoo wa machinjo

"watu wanatuona kama kondoo kwa ajili ya machinjo"

kondoo wa machinjo

Mwandishi anafananisha Waisraeli na kondoo ambao watu huua na kula. Kama kondoo wasivyojiweza mbele ya wale wanaowaua, hivyo ndivyo Waisraeli wasivyojiweza mbele ya adui zao.

Psalms 44:23

Amka, kwa nini unalala, Bwana?

Hii haimaanishi ya kuwa Mungu amelala kweli. Mwandishi anazungumzia Mungu kuonekana kama hatendi kitu kana kwamba amelala. Anauliza swali hili kumkemea Mungu kwa kuonekana kutokujali kuhusu taabu zao. "Amka! Naona kama umelala, Bwana!"

usitutupe

Mwandishi anamzungumzia Mungu kuikataa Israeli kwamba alikuwa akitupa nguo ambayo haitaki. "usitukatae"

Kwa nini unaficha uso wako ... kukandamizwa kwetu?

Mwandishi anatumia hili swali kulalamika kuwa Mungu anaonekana kutowajali. "Usifiche uso wako ... kukandamizwa kwetu."

unaficha uso wako

Mwandishi anasungumzia Mungu kutowajali kana kwamba Mungu alikuwa akificha uso wake ili asiwaone. "kutujali"

kusahau mateso yetu na kukandamizwa kwetu

Maneno "mateso" na "kukandamizwa " inamaanisha kitu kimoja na inaweka mkazo ya ukali wa mateso. "kusahau kuwa watu wanatutesana kutukandamiza" au "kusahau kuwa watu wanatutesa sana"

Psalms 44:25

Kwa kuwa tumeyeyuka kwenye mavumbi; miili yetu inang'ang'ania nchini

Misemo hii ya usambamba ina maana za kufanana. Mwandishi anaelezea watu wake kama wamelala ardhini katika mkao wa kushindwa na kudhalilishwa.

Kwa kuwa tumeyeyuka kwenye mavumbi

Mwandishi anazungumzia kudhalilishwa kwao kana kwamba miili yao ni vitu, kama barafu, inayoyeyuka na kulowa kwenye mchanga.

miili yetu inang'ang'ania nchini

Mwandishi anazungumzia kudhalilishwa kwao kana kwamba miili yao ilikuwa imekwama kwenye ardhi na hawakuweza kujinyanyua juu.

inuka

Hii ni amri ya kusimama. Msemo huu unamaanisha kuanza kutenda kitu. "Tenda jambo"

Psalms 45

Psalms 45:1

Taarifa ya jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

weka katika Shoshannimu

Hii inaweza kuwa mtindo wa mlio wa muziki. wakati mwingine inatafsiriwa kama "weka katika mlio wa 'yungiyungi.'"

Zaburi ya wana wa Kora

"Hii ni zaburi ambayo wana wa Kora waliandika."

Maschili

Hii inaweza kumaanisha mtindo wa muziki.

Wimbo wa upendo

"Wimbo wa mapenzi"

Moyo wangu umefurika kwa neno zuri

Mwandishi anazungumzia moyo wake kana kwamba ni chombo kinachofurika na kimiminiko. Neno "moyo" linawakilisha hisia zake, amabzo zinafurahishwa kwa nyimbo anazoimba. "Hisia zangu zinafuraha juu ya neno zuri"

neno zuri

"wazo lenye uadilifu." Hii inamaanisha wimbo alioandika.

niliyotunga

kuandika au kuunda wimbo

ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi aliye tayari

Mwandishi anazungumzia ulimi wake kana kwamba ni kalamu. Anazungumza kwa ujuzi kama mwandishi mwenye uzoefu anavyoandika. "ulimi wangu ni kama kalamu ya mtu anayeandika vizuri" au "ninapozungumza kwa ujuzi kama mwandishi mwenye uzoefu anavyoweza kuandika maneno"

Wewe ni mzuri kuliko watoto wa wanadamu

Msemo huu ni kukuza kwa neno na inasisitiza kuwa mfalme ni mzuri kwa mwonekano kuliko mtu mwingine. Msemo "watoto wa watu" ni lahaja inayomaanisha watu wote. "Una uzuri zaidi ya mtu mwingine yeyote"

neema imemwagwa katika midomo yako

Mwandishi anazungumzia neema kana kwamba ni mafuta ambayo mtu ametumia kuitia mafuta midomo yake. Neno "midomo" linamaanisha maneno ya mfalme. Msemo huu unamaanisha kuwa mfalme anazungumza kwa ufasaha. "ni kana kwamba mtu ametia mafuta midomo yako kwa mafuta" au "unazungumza kwa ufasaha"

Psalms 45:3

Weka upanda wako pembeni yako

Mashujaa walibeba mapanga yao katika makundi yalioning'inia kwenye mshipi katika viuno vyao. Upanga utakaa pembeni mwao. Msemo huu unaeleza tendo la mtu kujiandaa kwa ajili ya viti. "Jiandaeni kwa ajili ya vita"

uende kwa ushindi

Mwandishi anamwambia mfalme kumpanda farasi wake au kibandawazi kuelekea katika ushindi.

kwa sababu ya uaminifu, upole, na haki

Maana zinazowezekana ni 1) hizi ni sifa za mwenye nguvu. "kwa sababu u mwaminifu, mpole, na mwenye haki" au 2) sifa hizi anazopambana kushikilia kwa ajili ya watu anaowatawala. "ili kushika uaminifu, upole, na haki"

mkono wako wa kuume utakufundisha mambo ya kuogofya

Askari walio wengi walishikia mapanga yao kwa mkono wao wa kuume walipopigana, ambayo mwandishi anazungumzia kana kwamba ni mtu anayeweza kumfunza mfalme kupitia uzoefu anaopitia vitani. "Utajifunza kutimiza matendo makubwa ya kijeshi kwa kupigana katika vita nyingi"

mambo ya kuogofya

"matendo ya ajabu." Hii inamaanisha ushindi wa kijeshi unaowasababisha adui zake kumwogopa na rafiki zake kumheshimu sana.

Psalms 45:5

watu wanaanguka chini yako

Msemo huu unamaanisha mfalme kuwashinda adui zake. Maana zinazowezekana ni 1) "watu wanaanguka miguuni mwako kwa kusalimu amri" au 2) "watu wanaanguka wakiwa wamekufa miguuni mwako."

mishale yako iko mioyo ya adui wa mfalme

"mishale yako imechoma mioyo ya adui zako." Mwandishi anazungumza kwa mfalme huku akimweleza mfalme katika nafasi ya mtu wa tatu.

Kiti chako cha enzi ... ni wa milele na milele

maneno "Kiti chako cha enzi" yanawakilisha ufalme na utawala wa mfalme. "Ufalme wako ... ni wa milele na milele" au "Utatawala ... milele na milele"

Kiti chako cha enzi, Mungu

Maana zinazowezekana ni kwamba neno la "Mungu" 1) ni jina kwa ajili ya mfalme, ambaye ni mwakilishi wa Mungu au 2) linaboresha maneno "kiti cha enzi" na linamaanisha "Ufalme wako ambao Mungu amekupa"

fimbo ya hukumu ni fimbo ya ufalme wako

Neno "fimbo" linawakilisha mamlaka ya mfalme kutawala ufalme wake. "unatawala ufalme wako kwa haki"

Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta ya furaha

Mwandishi anazungumzia furaha kana kwamba ni mafuta ambayo Mungu alitumia kumtia mafuta mfalme. Mungu kumtia mafuta ni ishara inayowakilisha kwamba Mungu amemchagua kuwa mfalme. "Mungu alipokuchagua kama mfalme, alikufanya kuwa na furaha sana"

Psalms 45:8

Taarifa ya Jumla:

Hapa mwandishi anaanza kueleza kile kinachoonekana kuwa sherehe ya arusi ya mfalme na bibi arusi wake.

manemane, mshubiri ,na mdalasini

Hii ni mimea yenye harufu nzuri ambayo watu hutumia kutengeneza manukato.

majumba ya mapembe

Mapembe ni meno meupe magumu ya nje ya mnyama. Msemo huu unaelezea jumba lenye kuta na samani ambazo watu wamepamba kwa mapembe.

vyombo vya nyuzi vimekupa furaha

Maneno "vyombo vya nyuzi" yanamaanisha muziki ambao watu hutengeneza kwa kucheza vyombo vya nyuzi. "muziki wa vyombo vya nyuzi umekufanya kuwa na furaha"

wanawake wenye heshima

Hawa wanawake ni wake wa mfalme waliopokea kibali hiki.

malkia

Hii inamaanisha mwanamke atakaye kuwa malkia. "bibi arusi wako, malkia" au "bibi arusi wako, atakaye kuwa malkia"

Ofiri

Hili ni jina la sehemu iliyokuwa ikijulikana kwa dhahabu yake safi. " Mahali hapajulikani.

Psalms 45:10

Sikiliza, binti

Mwandishi anaanza kuzungumza na malkia na anamuita kama "binti" yake kwa sababu ni msichana mdogo.

tega sikio lako

Mwandishi anazungumzia kusikiliza kitu kwa makini kana kwamba ni kuinamisha sikio la mtu kuelekea kwa mtu anayezungumza. "sikiliza kwa makini"

wasahau watu wako mwenyewe

Mwandishi anamzungumzia malkia kuacha kufuata imani na desturi za watu wake wa asili kana kwamba ni kuwasahau. "usifuate tena desturi za watu wako"

nyumba ya baba yako

Hapa neno "nyumba" linamaanisha familia. "ndugu zako"

Katika njia hii

"na" au "kwa hiyo"

mfalme atatamani uzuri wako

Hii ni njia ya ustarabu ya kusema kuwa mfalme atataka kulala na malkia kama mke wake.

Psalms 45:12

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaendelea kuzungumza na malkia.

Binti wa Tiro

Mwandishi anazungumza na watu wanaoishi Tiro kana kwamba ni watoto wa Tiro. "Watu wa Tiro"

binti wa kifalme

Hii inamaanisha mwanamke ambaye mfalme atamuoa. "Bibi arusi wa mfalme"

amependeza

"mzuri sana." Hii inamaanisha mwonekano wa mwanamke.

mavazi yake yameundwa kwa dhahabu

Mavazi yake yamepambwa au kushonwa kwa dhahabu. "anavaa mavazi ambayo mtu ameshona kwa uzi wa dhahabu"

Psalms 45:14

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaendelea kuzungumza kuhusu malkia lakini anaanza kwa kuzungumza na mfalme kwanza.

Ataongozwa kwenda kwa mfalme na nguo ya tarizi

"Watu watamwongoza kwenda kwa mfalme akiwa amevaa nguo ya tarizi"

tarizi

mtindo ulioundwa kwa kushona nyuzi za rangi kwenye nguo

wanawali, wenzake wanaomfuata, wataletwa kwako

Hapa neno "kwako" inamaanisha mfalme. "watu watakuletea wanawali, wenzake wanaomfuata"

Wataongozwa kwa furaha na shangwe

Msemo huu unaeleza "furaha na shangwe" kama mtu anayewaongoza wengine kusherehekea. "Furaha na shangwe zitawaongoza" au "Wataenda kwa furaha na shangwe"

furaha na shangwe

Maneno haya mawili yana maana moja na yanasisitiza ukali wa furaha. "furaha kubwa"

Psalms 45:16

Kauli Unganishi:

Mwandishi anaendelea kuzungumza na mfalme.

Katika sehemu ya baba zako watakuwa watoto wako

Hii inamaanisha wana wa mfalme watachukua nafasi yake kama mfalme, kama yeye alivyochukua nafasi ya mababu zake.

utafanya wakuu duniani kote

Msemo "duniani kote" ni kukuza kwa neno kusisitiza kwamba atatawala juu ya mataifa mengi. "utafanya watawala juu ya mataifa mengi"

Nitalifanya jina lako likumbukwe katika vizazi vyote

Hapa "atakayefanya" ni mwandishi. Neno "jina" linamaanisha tabia ya mfalme na sifa yake. "Nitawasababisha watu katika kila kizazi kujua kuhusu ukuu wako"

Psalms 46

Psalms 46:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Zaburi ya wana wa Kora

"Hii ni zaburi ambayo wana wa Kora waliandika"

weka katika Alamothi

Hii inaweza kumaanisha aina ya muziki.

Mungu ni kimbilio letu na nguvu yetu

Mwandishi anamzungumzia Mungu kana kwamba ni sehemu ambapo watu wanaweza kwenda kwa ajili ya usalama. "Mungu hutupa ulinzi na nguvu"

milima itikiswe katika moyo wa bahari

Mwandishi anazungumzia kilindi cha chini zaidi ya bahari kana kwamba ni moyo wa bahari. Hapa anaelezea tetemeko la dunia linalo sababisha milima kumeng'enya na kuanguka baharini. "milima inatakiwa kutikisika kwa nguvu sana hadi ianguke kwenye vilindi vya bahari"

ingawa maji yake yanaunguruma na kukasirika

"ingawa maji ya bahari wanaunguruma na kukasirika." Maneno "kuunguruma" na "kukasirika" yanaelezea kusogea kwa nguvu kwa bahari wakati wa dhoruba kali.

milima inatetemeka katika kuvimba kwake

Msemo "kuvimba kwake" kinamaanisha maji ya bahari yanapoinuka na kugonga milima. "kuvimba kwa maji kunasababisha milima kutetemeka"

Psalms 46:4

Kuna mto, mikondo ambayo huufanya mji wa Mungu kuwa na furaha

"Kuna mto ambao mikondo yake huufanya mji wa Mungu kuwa na furaha." Hii picha ya mto unaotiririka inaashiria amani na mafanikio kwa ajili ya mji wa Mungu.

huufanya mji wa Mungu kuwa na furaha

Msemo "mji wa Mungu" unamaanisha yerusalemu, ambao mwandishi anauzungumzia kama mtu anayeweza kuwa na furaha. "huwafanya watu wanaoishi Yerusalemu kuwa na furaha"

sehemu takatifu za hema takatifu za Aliye juu

Msemo huu unaelezea "mji wa Mungu." Wingi wa mahema unaweka mkazo katika wazo kwamba hapa ni mahali patakatifu pa Mungu kuishi. "sehemu takatifu anapoishi Aliye juu"

katikati yake; hatasogezwa ... atamsaidia.

Panapozungumziwa na "mji wa Mungu."

hatasogezwa

Hapa neno "kusogezwa " ni sawa na neno linalotafsiriwa "kutikiswa" katika 46:1. Mwandishi anazungumzia uharibifu wa Yerusalemu kwa majeshi kana kwamba tetemekolingeuangamiza. "hakuna kitu kitakachoweza kuuangamiza"

Psalms 46:6

mataifa yalikasirika

Hapa neno "kukasirika" ni neno sawa mwandishi alilotumia katika 46:1 kuelezea maji ya bahari. Mwandishi anazungumzia uoga wa mataifa kana kwamba ni kusogea kwa fujo kwa bahari wakati wa dhoruba. "mataifa yanaogopa"

falme zilitikiswa

Hapa neno "kutikiswa" ni neno sawa ambalo mwandishi alitumia katika 46:1 kuelezea madhara ya tetemeko kwenye milima. Mwandishi anazungumzia kuangushwa kwa falme na majeshi kana kwamba tetemeko litawaangamiza. "majeshi yanapindua falme"

akainua sauti yake

"Mungu akainua sauti yake." Mwandishi anazungumzia "sauti" kana kitu amabcho mtu anaweza kuinua na kuweka hewani. Hii inamaanisha kwamba sauti inakua ya sauti zaidi. "Mungu alipaza sauti"

dunia ikayeyuka

Mwandishi anazungumzia dunia kama kitu, kama barafu, inayoweza kuyeyuka. Hapa "'dunia" inawakilisha binadamu, na kuyeyuka inawakilisha uoga. "watu wa duniani wanatetemeka kwa uoga"

Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu

Mwandishi anamzungumzia Mungu kana kwamba ni sehemu ambayo watu wanaweza kwenda kwa ajili ya ulinzi. "Mungu wa Yakobo anatupa ulinzi"

Mungu wa Yakobo

Maana zinazowezekana ni 1) "Mungu ambaye Yakobo alimwabudu" au 2) "Yakobo: ni njia nyingine ya kusema taifa la Israeli na inamaanisha "Mungu wa Israeli."

Psalms 46:8

Hufanya vita kukoma

"Hufanya mataifa kuacha kupigana vita"

hadi mwisho wa dunia

Huu ni msemo wa nahau unaomaanisha sehemu zote duniani. "sehemu zote duniani"

huvunja upinde ... huunguza ngao

Njia moja ambayo Yahwe atakomesha vita vyote kwa kuangamiza silaha ambazo majeshi hutumia kupigania.

Psalms 46:10

Kuwa kimya na ujue kuwa mimi ni Mungu

Hapa, Mungu anaanza kuzungumza.

Kuwa kimya

Katika hali hii, maneno haya yanawezekana kuwa ni amri kwa mataifa kukomesha vita vyao. "Acheni kupigana"

ujue kuwa mimi ni Mungu

Hapa neno "kujua" inamaanisha kuelewa na kukiri kuwa Yahwe ndiye Mungu wa kweli.

Nitatukuzwa katika mataifa; nitatukuzwa duniani

Misemo hii miwili inamaana sawa na inasisitiza kuwa watu wa kila taifa duniani watamtukuza Mungu. "Watu katika kila taifa watanitukuza; watu duniani kote watanitukuza"

Yahwe wa majeshi yuko nasi; Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu

Mwandishi anamzungumzia Mungu kana kwamba ni sehemu ambayo watu wanaweza kwenda kwa ajili ya ulinzi.

Psalms 47

Psalms 47:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Zaburi ya wana wa Kora

"Hii ni zaburi iliyoandikwa na wana wa Kora"

Piga makofi

Kupiga makofi inahiusishwa na sherehe. "Piga makofi kwa kusherehekea"

piga kelele kwa Mungu na sauti ya ushindi

piga kelele kwa Mungu na sauti za furaha." Hapa neno "ushindi" inamaanisha furaha inayohusiana na ushindi

Psalms 47:3

Anawatiisha watu chini yetu na mataifa chini ya miguu yetu.

Misemo hii miwili ina usambamba na inamaanisha kuwa Mungu aliwezesha Israeli kuwashinda adui zake.

Anawatiisha

Kushinda na kuweka chini ya mamlaka ya mwingine

chini yetu ... chini ya miguu yetu

Mwandishi anazungumzia kuyashinda mataifa mengine kana kwamba ilikuwa kuyaweka mataifa hayo chini ya miguu yao.

Anatuchagulia urithi wetu

Mwandishi anazungumzia nchi ya Israeli kana kwamba ilikuwa ni urithi ambao Mungu aliwapa watu kama mali ya milele. "Anachagua nchi hii kama urithi wetu"

utukufu wa Yakobo

Hapa neno "utukufu" inmaanisha chanzo cha majivuno na linaashiria nchi ambayo Mungu amewapa watu wake kama urithi. "nchi ambayo Yakobo anajivunia"

Yakobo aliyempenda

Neno "Yakobo" linaashiria taifa la Israeli.

Mungu ameenda juu kwa shangwe

Mwandishi anamzungumzia Mungu kuyashinda mataifa kana kwamba Mungu alikuwa mfalme anaye panda kwenye kiti chake cha enzi, kilicho kuwa hekaluni. "Mungu ameenda juu kwenye hekalu wakati watu wakipiga shangwe" (UDB) au "Mungu amepanda kwenye kiti chake cha enzi wakati watu wakipiga shagngwe"

Yahwe kwa sauti ya tarumbeta

Msemo huu uko sambamba na msemo uliopita. Kitenzi kinaweza kuwekwa kuweka wazi. "Yahwe ameenda juu wakati watu wakipuliza tarumbeta"

Psalms 47:6

Mwimbieni sifa Mungu, imbeni sifa; imbeni sifa kwa mfalme wetu, imbeni sifa

Msemo "imbeni sifa" unarudiwa kwa ajili ya msisitizo. "Mwimbieni, mwimbieni sifa Mungu; imbeni, imbeni sifa kwa mfalme wetu"

Psalms 47:8

Wakuu wa watu

"Viongozi wa mataifa yote"

wamekusanyika pamoja kwa watu

Maana zinazowezekana ni kwamba watawala wa mataifa 1) "wanakusanyika mbele ya mataifa" (UDB) au 2) "walikusanyika pamoja na watu" ili wote wamwabudu Mungu kama mfalme.

ngao za ulimwengu ni za Mungu

Maana zinazowezekana ni kwamba "ngao" 1) zinamaanisha vifaa vya vita. "Mungu ana uwezo zaidi ya silaha za wafalme wote dunia" (UDB) au 2) inamaanisha viongozi wa mataifa ambao wanazungumzia kama ngao ambazo zinalinda mataifa yao. "wafalme wa duniani wako chini ya Mungu"

Psalms 48

Psalms 48:1

Taarifa ya Jumla:

Huu ni wimbo kuhusu Yerusalemu kuwa sehemu ya kuishi ya Mungu.

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

zaburi ya wana Kora

"hii ni zaburi ambayo wana wa Kora waliandika"

mwenye kusifiwa sana

"watu wanapaswa kumsifu sana"

mji wa Mungu wetu katika mlima wake mtakatifu

Hii inamaanisha Yerusalemu, iliyojengwa katika mlima Sayuni.

mji wa Mungu wetu

Maana zinazowezekana ni 1) "mji ambao Mungu wetu huishi" au 2) "mji ulio wa Mungu wetu"

Mzuri katika kuinuka

"Mzuri na juu." Neno "kuinuka" linamaanisha jinsi mlima Sayuni ulivyo juu.

furaha ya dunia yote, ni mlima Sayuni

Hapa neno "dunia" linamaanisha kila mtu anayeishi duniani. "Mlima Sayuni huwapa watu wote duniani furaha" au "watu wote wanafurahi kwa sababu ya mlima Sayuni"

katika pande za kaskazini

Maana zinazowezekana ni kwamba msemo huu 1) unamaanisha mwelekeo wa kaskazini au 2) ni jina jingine la mlima sayuni linalomaanisha "mlima wa Mungu."

Mungu amejifanya kujulikana katika majumba yake kama sehemu ya kukimbilia

Mwandishi anamzungumzia Mungu kana kwamba ni sehemu ambapo watu wanaweza kwenda kwa ajili ya usalama. "Mungu amejifanya kujulikana kama yule anayetoa usalama kwa watu katika majumba ya mlima Sayuni"

Psalms 48:4

tazama

Neno "tazama" hapa linataka tuwe macho na kuzingatia taarifa ya kushangaza inayofuata.

wamejikusanya

Hii inamaanisha kwamba wafalme wa mataifa walikusanya majeshi yao. "walikusanya majeshi yao"

wakapita pamoja

"kwa pamoja walipita Yerusalemu"

Wakaona

"Wakaona Yerusalemu"

hawakufadhaika

"taabika sana"

Kutetemeka kuliwashika

Mwandishi anazungumzia hofu ya wafalme kana kwamba ni mtu aliyesababisha wafalme na majeshi yao kutetemeka. "Huko walitetemeka kwa hofu"

maumivu kama ya mwanamke mwenye uchungu wa kuzaa

Mwandishi anazungumzia hofu ya wafalme kana kwamba ni maumivu ambayo mwanamke hupitia wakati wa kuzaa na kuzungumzia maumivu haya kana kwamba ni mtu. "maumivu yaliwashika, kama mwanamke aliye katika uchungu wa kuzaa" au "wakaogopa, kama mwanamke anavyoogopa kupitia maumivu ya kuzaa"

Psalms 48:7

Na upepo wa mashariki unavunja meli za Tarshishi

Maana zinazowezekana ni 1) hii ni sitiari ambayo mwandishi anawaelezea wafalme kuwa na hofu kana kwamba ni meli zinazotikisika kwa sababu Mungu anaziangamiza kwa upepo mkali. "Walitikisika kwa hofu, kama meli za Tarshishi zinavyotikisika unapozivunja na upepo wa mashariki" au 2) hii ni alama ya kifupisho ambayo mwandishi anaelezea nguvu kuu ya Mungu.

upepo wa mashariki

Maana zinazowezekana ni 1) "upepo unaopuliza kutoka mashariki" au 2) "upepo mkali."

meli za Tarshishi

Maana zinazowezekana ni kuwa hii inamaanisha 1) meli zinazosafiri kwenda Tarshishi au zimetengenezwa katika mji wa Tarshishi au 2) meli yoyote kubwa ya kwenda baharini.

Kama tulivyosikia

Inadokezwa kuwa kile walichosikia ni mambo makubwa ambayo Mungu ametenda kipindi cha nyuma. "Kama tulivyosikia kuhusu mambo makubwa ambayo Mungu ametenda"

ndivyo tulivyoona

Hii inamaanisha kuwa wameona kithibitisho kuwa vitu walivyosikia ni vya kweli. "kwa hiyo tumeona Mungu akifanya mambo makuu sasa"

katika mji wa Yahwe wa majeshi, katika mji wa Mungu wetu

Misemo hii miwili inamaanisha Yerusalemu. "katika mji wa Mungu wetu, Yahwe wa majeshi"

imarisha

"ifanye kuwa imara." Hapa neno "imarisha" linamaanisha kutunza na kufanya kitu kuwa salama.

Psalms 48:9

katikati ya hekalu lako

"kama tulivyo kwenye hekalu lako"

Kama jina lako lilivyo ... ndivyo ilivyo sifa yako hadi mwisho wa dunia

Hapa neno "jina" linawakilisha tabia ya Mungu na sifa yake. Misemo hii miwili inalinganisha ukuu wa sifa ya Mungu na jinsi watu wanavyomsifu sana. "Jina lako ni kuu sana ... na kwa hiyo watu duniani kote wanakusifu sana" au "Watu duniani kote wamesikia kukuhusu ... kwa hiyo watu duniani kote wanakusifu"

hadi mwisho wa dunia

Huu ni msemo wa nahau unaomaanisha sehemu zote duniani.

mkono wako wa kuume umejaa haki

Mwandishi anazungumzia haki kana kwamba ni kitu ambacho Mungu anaweza kushika mkononi mwake. Hapa neno "mkono" unamaanisha uwezo na mamlaka ya Mungu kutawala. "unatawala kwa haki" au "wewe ni mwenye haki unapotawala"

Psalms 48:11

Acha mlima Sayuni ufurahi

Mwandishi anazungumzia mlima Sayuni kana kwamba ni mtu anayeweza kufurahi. Msemo unamaanisha watu wanaoishi Yerusalemu. "Acha wale wanaoishi mlima Sayuni wafurahi"

acha binti wa Yuda wafurahi

Mwandishi anazungumzia miji ndani ya Yuda kana kwamba ni watoto wa Yuda. Msemo huu unamaanisha watu wanaoishi katika miji hio. "acha watu wanaoishi katika miji ya Yuda wafurahi"

Psalms 48:12

Tembeeni katika mlima Sayuni, mzungukeni

Misemo hii miwli ina usambamba. "Tembeeni kote mkiuzunguka mlima Sayuni"

angalieni vizuri

"angalieni kwa umakini"

Psalms 48:14

atakuwa mwongozo wetu

"atatuongoza"

hadi kifo

Maana zinazowezekana ni 1) "hadi tufe" au 2) "milele."

Psalms 49

Psalms 49:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Zaburi ya wana wa Kora

"Hii ni zaburi ambayo wana Kora waliandika"

Sikieni haya, enyi watu wote; toeni maskio, wakazi wote

Misemo hii miwili ina usambamba. Kwa pamoja inaimarisha amri kwa watu wote kusikiliza.

toeni maskio

Huu ni msemo wa nahau unaomaanisha kutumia maskio kusikiliza. "sikilizeni"

wote wa chini na juu

Mwandishi anazungumzia watu walio wanyonge au wasio wa muhimu katika jamii kama kuwa chini na watu walio muhimu na wenye uwezo kama kuwa juu. Kwa pamoja, maneno "chini" na "juu" wanawakilisha watu wote. "wote watu muhimu na watu ambao sio wa muhimu" au "watu wa daraja katika jamii"

tajiri na maskini pamoja

Kwa pamoja, maneno "tajiri" na "maskini" yanamaanisha watu wote, bila kujali mali. "watu wote"

Psalms 49:3

Mdomo wangu utazungumza hekima

Hapa neno "mdomo" inamaanisha mtu anayezungumza. "Nitazungumza maneno ya hekima"

kutafakari kwa moyo wangu kutakuwa kwa uelewa

Hapa neno "moyo" linawakilisha akili na mawazo. "mawazo ambayo ninatafakari yatanielekeza kwenye uelewa"

tega sikio langu

Mwandishi anazungumzia kusikiliza kitu kwa makini kana kwamba ni kuinamisha sikio la mtu kwa mtu anayezungumza. "sikiliza kwa makini"

kwa kinubi

"kama ninavyocheza kinubi"

Kwa nini niogope ... visigino vyangu?

Mwandishi anatumia wali hili kuweka mkazo kwamba hakuna sababu ya kuogopa vitu vibaya vinapotokea. "Sina sababu ya kuogopa ...visigino vyangu."

siku za uovu

"vitu viovu vikitokea." Hapa neno "siku" linamaanisha nyakati kwa ujumla.

udhalimu unaponizunguka katika visigino vyangu

Maana zinazowezekana ni 1) mwandishi anazungumzia hamu za uovu za adui zake kana kwamba ni mnyama anayewinda wanyama wengine aliye tayari kumpita. "wakati udhalimu wa watu wenye dhambi unapokuwa tayari kunishinda" au 2) adui wa mwandishi wanamzunguka wakati wanatenda udhalimu wao. "adui zangu wanaponizunguka"

Psalms 49:6

wale wanaotumaini katika mali zao

Watu hawa wanatumaini kuwa mali zao zitawaepusha na mateso.

kuhusu kiasi cha utajiri wao

kiasi kikubwa cha kitu

Ni hakika kuwa hakuna mtu

"Hakuna namna ambayo yeyote anaweza" au "Hakuna anayeweza"

hakuna mtu anayeweza kumkomboa ndugu yake au kumlipa Mungu kwa ajili yake

Misemo yote hii inaeleza kuwa mtu hawezi kumpa Mungu fedha ya kutosha ya kuepuka kifo. "hakuna mtu anayeweza kulipa fedha kwa Mungu ili ndugu yake asife"

ukombozi wa maisha ya mtu ni gharama

"inagharimu sana kukomboa maisha ya mtu"

Psalms 49:9

ili mwili wake usioze

Hii inamaanisha mwili kuoza katika kaburi.

ataona uozo

Mwandishi anazungumzia kupitia kitu kana kwamba ilikuwa ni kukiona hicho kitu. "atakufa na mwili wake kuoza"

Watu wenye hekima hufa; mpumbavu na mjinga wote wanaangamia

Mwandishi anamaanisha watu wote kwa kuwataja wale walio na hekima nyingi zaidi na kidogo zaidi.

mjinga

mtu ambaye hajui kitu

Psalms 49:11

Mawazo yao ya ndani

"Imani yao"

nasehemu wanazoishi, kwa vizazi vyote

"na sehemu wanazoishi zitaendelea vizazi vyote"

wanaita ncho baada ya majina yao

"wanaita nchi zao kwa majina yao wenyewe." "wanamiliki nchi zao wenyewe"

Psalms 49:12

Lakini mtu, akiwa na mali

"Lakini mtu, hata kama ana mali"

Hii, njia yao, ni upuuzi wao

Mwandishi anazungumzia hatima ya wapumbavu kana kwamba ni mwisho wao katika njia wanayotembea. "Hii ndio hatima ya wale wanaotenda upuuzi"

lakini baada yao

"lakini baada ya kufa"

Psalms 49:14

Taarifa ya jumla:

Mwandishi anaendelea kuwaelezea watu wanaoamini kuwa mali yao itawaokoa.

Kama kondoo

Mwandishi anawafananisha watu watakaokufa kama kundi la kondoo. Kama kondoo amabvyo hawawezi kutoroka wakati bucha anapoamua kuwachinja, kwa hiyo watu hawatatoroka ukifika wakati wao kufa.

wamechaguliwa

"Mungu amewachagulia"

mauti itakuwa mchungaji wao

Mwandishi anazungumzia watu kufa kwa kutaja mauti kama mtu ambaye ni mchungaji anayewaongoza katika kaburi. "mauti itawapeleka kama mchungaji anavyowaongoza kondoo kwenda machinjioni"

asubuhi

Hapa neno "asubuhi" ni sitiari inayomaanisha wakati ambapo Mungu atawathibitisha watu wenye haki na kuwaokoa kutoka kwa watu waovu.

miili yao itamezwa kuzimu

Mwandishi anazungumzia kuzimu, sehemu ya wafu, kana kwamba ni mtu au mnyama. Anazungumzia uozo wa miili iliyokufa kana kwamba kuzimu inaila. "miili yao itaoza kaburini"

Mungu atakomboa maisha yangu kutoka kwenye nguvu ya kuzima

Mwandishi anazungumzia kuzimu kana kwamba ni mtu aliye na nguvu juu ya wale walio kufa. Kutokana na muktadha, inadokezwa kwamba uwezo huu unamaanisha kuteketeza miili ya wafu.

Mungu atakomboa maisha yangu

Hapa neno "maisha" linamaanisha mtu mzima. "Mungu atanikomboa"

Psalms 49:16

utukufu wa nyumba yake unaongezeka

neno "utukufu" hapa unamaanisha mali au utajiri. Maana zinazowezekana ni 1) "atakapopata utajiri zaidi katika nyumba yake" au 2) "familia yake inapokuwa tajiri zaidi."

hatachukua kitu

"hatachukua kitu chochote kwenda nacho kaburini"

utukufu wake hautamfuata chini

Msemo "kwenda chini" unamaanisha wakati mtu anapokufa. "utukufu wake hautamfuata atakapokufa" au "hatatunza sifa yake atakapokufa"

Psalms 49:18

Akabariki nafsi yake

Hapa neno "nafsi" linamaanisha mtu mzima. Msemo huu unamaanisha kuwa alijiona kuwa na furaha na mafanikio kwa sababu ya utajiri wake. "Akajipongeza mwenyewe"

na watu wanakusifu unapoishi kwa ajili yako mwenyewe

Hapa mwandishi anatoa kauli ya ujumla kuhusu jinsi watu wanavyozungumza kuhusu watu wengine waliofanikiwa kulingana na mtazamo wa kidunia.

unapoishi kwa ajili yako mwenyewe

Msemo huu unamaanisha kuishi kwa mafanikio kulingana na mtazamo wa kidunia. "fanya vyema kwa ajili yako" au "ishi kwa mafanikio"

ataenda katika kizazi cha baba zake

"ataenda mahali kizazi cha baba yake kilipo." Hii ni tasifida inayomaanisha kwamba mtu tajiri atakufa na kuungana na mababu zake kaburini. "ataungana na mababu zake kaburini"

hawataona nuru tena

wale ambao "hawataona" ni mtu tajiri na mababu zake. Neno "nuru" inaweza kuwa inamaanisha jua au ni sitiari ya uhai. "hawataliona jua tena" au "hawataishi tena"

Psalms 50

Psalms 50:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Taarifa ya Jumla:

Zaburi hii ni wimbo unaofundisha watu.

Zaburi ya Asafu

"Hii ni zaburi ambayo Asafu aliandika."

Mwenye nguvu, Mungu, Yahwe

Mwandishi anatumia majina matatu tofauti kumzungumzia Mungu.

akaiita dunia

Hapa neno "dunia" inamaanisha watu ambao wanaishi duniani. "akawaita watu wote"

kutoka kuchomoza kwa jua hadi kuzama kwake

Msemo huu unamaanisha upande wa mashariki, ambapo jua huchomoza, na magharibi, ambapo jua huzama. Mwandishi anatumia tofauti hizi mbili kuwakilisha sehemu zote duniani. "kila sehemu duniani"

Sayuni, ukamilisho wa uzuri

Maana zinazowezekana 1) "Sayuni, ambayo uzuri wake ni kamili" au 2) "Sayuni, mji mzuri zaidi."

Mungu ameng'aa

Mwandishi anamzungumzia Mungu kana kwamba ni nuru inayong'aa. Hii inamaanisha Mungu kusababisha watu kujua kuhusu utukufu wake. "Utukufu wa Mungu unang'aa kama taa"

Psalms 50:3

habaki kimya

Mwandishi anatumia kauli hii hasi kusisitiza kitu chanya. "huzungumza ili kila mtu aweze kumsikia"

moto unameza mbele yake

Mwandishi anazungumzia moto kuunguza vitu kana kwamba ulikuwa ukiwala. "moto unachoma mbele yake"

kuna tufani inayomzunguka

"kuna tufani kubwa imemzunguka"

Huita mbingu juu na dunia

Maana zinazowezekana ni 1) Mungu anawaita wote wanaoishi mbinguni na duniani kuwa mashuhuda akiwa anawahukumu watu wake au 2) Mungu anazungumza na mbingu na dunia kana kwamba ni watu, na anawaita kuwa mashahidi wakati anawahukumu watu wake.

Psalms 50:6

Mbingu zitatangaza

Maana zinazowezekana ni 1) mwandishi anatumia neno "mbingu" kumaanisha malaika wanaoishi huko. au 2) mwandishi anazungumzia "mbingu" kana kwamba ni mtu anayeshuhudia kuhusu haki ya Mungu.

Psalms 50:7

Sita kulaumu kwa sadaka zako

"Nitakulaumu, ila sio kwa sadaka zako." Mungu anaeleza kuwa sadaka zao sio sababu ya kuwalaumu.

laumu

"kemea" au "karipia"

sadaka zako za kuteketeza daima ziko mbele yangu

Hii inaelezea kwa nini Mungu hawalaumu kwa ajili ya sadaka zao. Msemo huu " daima ziko mbele yangu" unamaanisha kuwa katika uwepo wa Mungu na unamaanisha kuwa watu wake daima wanatoa sadaka zao cha kuteketeza kwake. "huwa mnatoa sadaka zenu za kuteketeza kwangu"

Psalms 50:9

mazizi

"kizimba"

ng'ombe kwenye vilima elfu

Msemo "kwenye vilima elfu" haiwakilishi idadi kamili ya ng'ombe ambazo Mungu anamiliki. Namba ni kukuza kwa neno ambayo inasisitiza kuwa Mungu anamiliki ng'ombe wote duniani. "ng'ombe wote duniani ni wangu"

vilima elfu

"vilima 1,000"

Nawajua ndege wote

Hapa neno "nawajua" inadokeza umiliki. "Ninamiliki ndege wote"

Psalms 50:12

Kama nina njaa

Hii inaelezea kitu ambacho hakiwezi kutokea, kwa kuwa Mungu huwa hapati njaa.

Je! Nitakula nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi?

Mungu anauliza swali hili balagha kusisitiza kuwa huwa hafanyi hivi vitu na kwa hiyo haitaji sadaka zao. "Sili nyama ya mafahali au kunywa damu ya mbuzi."

Psalms 50:14

Mtolee Mungu

Hapa Mungu inamaanisha mwenyewe. "Nitolee mimi"

lipi nadhiri zako kwa Aliye juu

Mwandishi anazungumzia "nadhiri" kana kwamba ni fedha ambayo mtu analipa kwa Mungu. "timiza nadhiri zako kwa Aliye juu" au "fanya kile ulichomwahidi aliye juu kufanya"

katika siku ya shida

Hapa neno "siku" linamaanisha wakati wowote. "unapokuwa na taabu"

Psalms 50:16

Lakini kwa waovu Mungu anasema

Hapa Mungu bado anazungumza na anajizungumzia mwenyewe katika hali ya mtu wa tatu. "Lakini kwa waovu nasema"

kwa waovu

Neno "waovu" inamaanisha watu waovu kwa ujumla. "kwa watu waovu"

Una nini na kutangaza sheria zangu ... na kutupa maneno yangu?

Mungu anatumia swali hili kukemea watu waovu. Swali hili linaweza kugeuzwa kuwa kauli. "Haina maana kwamba unatangaza sheria na agano langu, kwa kuwa unachukia maagizo yangu na kutupa maneno yangu." au "Sio sawa kwako kutangaza sheria zangu"

kwamba umechukua agano langu mdomo mwako

Mungu anazungumzia watu waovu kutongoa maneno ya agano kana kwamba wanaweka agano midomoni mwao. "kuzungumza kuhusu agano langu"

kutupa maneno yangu

Mungu anazungumzia watu waovu kukataa anachosema kana kwamba walikuwa wakitupa nje takataka. "kukataa ninachosema"

Psalms 50:18

unakubaliana naye

Maana zinazowezekana ni 1) kwamba wanakubaliana na matendo ya mwizi. "unamkubali" au 2) kwamba wanamuunga mwizi katika matendo yake. "unamuunga"

Unatoa mdomo wako kwa uovu

Mungu anamzungumzia mtu kuongea vitu vya uovu kana kwamba mdomo wa mtu ni mjumbe ambaye mtu anamtuma kufanya vitu viovu. "Daima huwa unasema vitu viovu"

ulimi wako unaeleza uongo

Neno "ulimi" linawakilisha mtu anayezungumza. "huwa unasema uongo daima"

Unakaa na kuzungumza dhidi ya ndugu yako; unamkashifu mtoto wa mama yako

Misemo hii miwili ina maana moja lakini inatumia maneno tofauti. Mungu anawashtaki kwa kuongea uongo dhidi ya watu wa familia yao wenyewe.

Unakaa na kuzungumza

"Kukaa na kuzungumza" dhidi ya mtu inaashiria kuwa mtu huyu anawaza kwa makusudi vitu vibaya vya kusema kwa mtu. "Huwa unawaza namna ya kuongea"

Psalms 50:21

ulifikiri kuwa mimi ni mtu kama wewe

kwa kuwa Mungu amekaa kimya na bado hajawakemea watu waovu kwa matendo yao, walidhani kuwa Mungu amekubaliana na walichofanya. "ulifikiri kuwa mimi ni mtu nayetenda kama nyie"

shutumu

"kemea" au "karipia"

kuleta ... vitu vyote ulivyofanya

Mungu anazungumzia kuorodhesha mambo maovu yote waliyotenda. "orodhesha ... vitu vyote mlivyofanya"

mbele ya macho yako

Hapa, kuwa "mbele ya macho yako" inamaanisha kuwa ni sehemu wanayoweza kuona. Hii inamaanisha kuwa hawataweza kukana mashtaka ambayo Mungu anawaletea. "mbele yenu" au "ili usiweze kuyakana"

nyie mnaomsahau Mungu

Mungu anawazungumzia waovu kumkataa kana kwamba wamemsahau. "Anajizungumzia katika hali ya mtu wa tatu. "nyie mlio nikataa"

nitawararua katika vipande

Mungu anazungumzia kuwaangamiza waovu kana kwamba ni simba anakula mawindo yake. "nitakuangamiza"

Psalms 50:23

hupanga njia yake katika namna sahihi

Mungu anazungumzia jinsi mtu anavyoishi kana kwamba ni njia ambayo mtu anasafiri. "huishi maisha yake katika njia sahihi"

Nitaonesha wokovu wa Mungu

Hapa Mungu anazungumzia kumwokoa mtu kana kwamba ilikuwa ni kumsababisha mtu kuona wokovu wake. Anajizungumzia katika hali ya mtu wa tatu. "Nitamwokoa"

Psalms 51

Psalms 51:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Taarifa ya Jumla:

Katika zaburi hii Daudi anamwomba Mungu msamaha.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

wakati nabii Nathani alipokuja kwake

Inaweza kuelezwa wazi Nathani alifanya nini alipokuja kwa Daudi, kwa sababu zaburi hii ni majibu ya hayo. "wakati nabii Nathani alipokuja kwa Daudi na kumkemea"

alipolala na Bathsheba

"baada ya Daudi kulala na Bathsheba"

kwa ajili ya umati wa matendo yako ya huruma

"kwa sababu unafanya mambo mengi sana ya huruma"

weka doa makosa yangu

Kusamehe dhambi inazungumziwa kana kwamba ni kati ya 1) kuwekea doa au 2) kufuta kumbukumbu za dhambi. "samehe dhambi zanguu kama mtu anazifuta" au "sahau dhambi zangu kama mtu anayefuta kumbukumbu za dhambi"

Nioshe kikamili kutokana na udhalimu wangu ... nisafishe na dhambi zangu

Misemo hii miwili inamaanisha kitu kimoja.

Nioshe kikamili kutokana na udhalimu wangu

Kukubaliwa na Mungu kunazungumziwa kama kuwa msafi. Mungu huwafanya watu kukubalika kwa kusamehe dhambi zao. "Osha dhambi zangu zote" au "Samehe dhambi zangu zote ili nikubalike kwako"

kikamili

"kikamilifu"

nisafishe na dhambi zangu

Kukubalika kwa Mungu kunazungumziwa kama kuwa msafi. Mungu huwafanya watu kukubalika kwa kusamehe dhambi zao. "Nifanye kuwa msafi na dhambi yangu" au "nisamehe kwa dhambi yangu ili niwe msafi"

Psalms 51:3

dhambi yangu daima iko mbele yangu

Kutoweza kusahau dhambi zake inazungumziwa kana kwamba zilikuwa mbele yake wakati wote ambapo anaweza kuziona. "huwa nina ufahamu wa dhambi zangu" au "siwezi kusahua dhambi zangu"

na kufanya kilicho kiovu mbele yako

"na nimefanya kilicho kiovu"

Psalms 51:5

Tazama, nilizaliwa katika udhalimu ... tazama, unatamani uaminifu

Matumizi mawili ya "Tazama" hapa yanavuta nadhari kati ya tofauti ya mambo haya mawili. "Hakika nilizaliwa katika udhalimu ... Lakini unatamani uaminifu"

Tazama, nilizaliwa katika udhalimu ... mara tu mama yangu alipochukua mimba yangu, nilikuwa katika dhambi

Misemo hii miwili inamaana moja na inatumika pamoja kuleta msisitizo.

nilizaliwa katika udhalimu

Kuwa mwenye dhambi inazungumziwa kama kuwa kwenye udhalimu. "nilikuwa mwenye dhambi tayari wakati nazaliwa"

mara tu mama yangu alipochukua mimba yangu, nilikuwa katika dhambi

Kuwa mwenye dhambi inazungumziwa kama kuwa kwenye dhambi. "hata mama yangu alipobeba mimba yangu, nilikuwa mwenye dhambi"

unatamani uaminifu moyoni mwangu

Moyo unawakilisha kati ya 1) hamu za mtu au 2) mtu mzima. "Unataka nitamani uaminifu" au "unataka niwe mwaminifu"

Psalms 51:7

Nitakase ... nitakuwa msafi ... nioshe ... nitakuwa mweupe zaidi ya theluji

Kukubalika kwa Mungu kunazungumziwa kama kuwa msafi au mweupe. Mungu huwafanya watu kukubalika kwa kusamehe dhambi zao.

Nitakase kwa hisopo

Mwandishi anamzungumzia Mungu kana kwamba Mungu ni kuhani ambaye humwaga maji juu yake kumfanya akubalike kwa Mungu. "Nifanye nikubalike kwa kunimwagia maji na hisopo" au "Nisamehe kwa dhambi zangu ili nikubalike kwako"

hisopo

Huu ni mmea ambao kuhani alitumia kunyunyizia maji au damu juu ya watu au vitu kuvifanya visafi kiutaratibu, yaani, kukubalika kwa Mungu.

mweupe zaidi ya theluji

Kutokuwa na dhambi kunazungumziwa kama kuwa mweupe. "mweupe sana"

furaha na shangwe

Maneno haya mawili yana maana moja na yana sisitiza hamu yake kusikia mambo ya furaha.

ili kwamba mifupa uliyovunja ifurahi

Kujisikia huzuni kali inazungumziwa kana kwamba mifupa yake imevunjika. "Kwa kuwa umesababisha huzuni kali ndani yangu. Acha nifurahi tena!"

Ficha uso wako mbali na dhambi zangu

Kufikiria kuhusu dhambi za mtu inazungumziwa kama kuziona. Kusamehe au kukataa kuwaza kuhusu dhambi inazungumziwa kama kuchagua kutoziona. "Usizitazame dhambi zangu" au "Usikumbuke dhambi zangu"

wekea doa udhalimu wangu

Kusamehe au kukataa kuwaza kuhusu dhambi inazungumziwa kama kati ya 1) kuziwekea doa au 2) kufuta kumbukumbu iliyoandikwa ya dhambi. "samehe dhambi zangu kama mtu anafuta kitu" au "samehe dhambi zangu kama mtu anayefuta kumbukumbu ya dhambi"

Psalms 51:10

Umba ndani yangu moyo msafi

Hapa "moyo" unawakilisha hisia na hamu. Kujitoa kamili na kuwa mtiifu kwa Mungu inazungumziwa kama na kuwa na moyomsafi. "Unifanye nijitoe kamili kwako" au "Nifanye nitake kukutii wewe daima"

fanya upya roho safi ndani yangu

Hapa "roho" inawakilisha mtazamo na hamu za Daudi. "fanya mtazamo wangu kuwa sawa" au "nifanye nitake daima kufanya kilicho sawa"

Usiniondoe mbali na uwepo wako

"Usinilazimishe kwenda mbali na wewe." Kukataliwa na Mungu kunazungumziwa kama kulazimishwa kwendambali naye. "Usinikatae mimi kama mmoja wa watu wako"

Psalms 51:12

na uniendeleza

"na unishike" au "unisaidie"

njia zako

"jinsi unavyotaka watu waishi" au "unachotaka watu wafanye"

watenda makosa ... watenda dhambi

Maneno haya mawili yanamaanisha watu wale wale.

Psalms 51:14

kumwaga damu

Msemo huu unamaanisha kumua mtu mwingine.

Bwana, fungua midomo yangu, na mdomo wangu utaeleza sifa yako

Kuwa na uwezo wa kuongea inazungumziwa kama midomo kuwa wazi. Hapa kutoweza kuongea ni ishara ya kuwa na hatia ya dhambi na kutoweza kujitetea. "Bwana, nifanye niweze kuongea, na nitakusifu"

hupendezwi na sadaka ... hauna furaha na sadaka za kuteketeza

Hii inamaanisha kwamba Mungu anataka kitu cha muhimu zaidi ya hivi vitu. "Sadaka haitoshi kukupendeza ... unataka kitu zaidi ya sadaka za kuteketeza"

Psalms 51:17

Sadaka za Mungu

"Sadaka zinazompendeza Mungu"

roho iliyovunjika

Roho iliyovunjika inawakilisha mtazamo wa unyenyekevu. "unyenyekevu" au "mtu anayekuwa mnyenyekevu"

moyo ulio vunjika na wenye majuto

Kuwa mnyenyekevu na majuto juu ya dhambi za mtu inazungumziwa kama kuwa na moyo ulio vunjika na wa majuto. Moyo unawakilisha hisia na nia. "huzuni na unyenyekevu" au "mtu anayejuta kwa ajili ya dhambi zake na ni mnyenyekevu"

uzijenge kuta za Yerusalemu

Kuta za mji huulinda mji na watu waliomo. Maana zinazowezekana ni 1) "utuwezeshe kujenga kuta za Yerusalemu" au 2) "ilinde Yerusalemu na uifanye kuwa imara"

watu wetu watatoa mafahali katika madhabahu yako

Fahali ni ng'ombe dume. Mafahali mara nyingi hutumika kama wanyama wa sadaka, kulingana na maagizo ya Mungu.

Psalms 52

Psalms 52:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Taarifa ya Jumla:

Katika zaburi hii anayezungumziwa ni Doegi. Wakati Sauli alipotaka kumuua Daudi, Doegi alimwambia Sauli mahali alipokuwa Daudi ili Sauli ampate.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Maschili

Hii inaweza kumaanisha mtindo wa muziki.

Doegi ... Mwedomi

Haya ni majina ya wanaume.

Kwa nini unajivunia kufanya fujo, wewe mwanamme shujaa?

Swali hili linaonesha jinsi Daudi alivyokuwa na hasira na yule aliyeleta matatizo. "Hutakiwi kuwa na majivuno sana kwa kutengeneza matatizo, wewe mwanamme shujaa."

wewe mwanamume shujaa

Inawezekana Daudi alikuwa akitumia kejeli alipokuwa anamwita Doegi hivi. "wewe, unadhani una uwezo sana"

Uaminifu wa agano wa Mungu unakuja

Daudi anazungumzia uaminifu wa Mungu wa agano kana kwamba ni kitu kilichoweza kuja. Inawezekana alikuwa akimaanisha ahadi za Mungu kuwalinda watu wake na watu waovu. Hii inaweza kuelezwa wazi. "Mungu ni mwaminifu kutunza ahadi za agano lake" au "Mungu huwalinda kwa uaminifu watu wake kutoka kwa watu waovu kama wewe"

wembe mkali

ubapa mkali

Ulimi wako unapanga maangamizi kama wembe mkali, unafanya udanganyifu

Hapa ulimi unalinganishwa na wembe mkali ambao unauwezo wa kusababisha madhara makubwa. "Ulimi wako unadhuru watu kama wembe mkali ufanyavyo, unapopanga maangamizi na kudanganya wengine"

Ulimi wako

Hapa "ulimi wako" unaashiria mtu ambaye Daudi anazungumza naye. "Wewe"

Psalms 52:3

Kauli Unganishi:

Daudi anaendelea kuzungumza na "mwanamme shujaa" wa 52:1

kudanganya kuliko kuzungumza haki

"unapenda kudanganya zaidi ya kusema kilicho sawa"

Psalms 52:4

maneno yanayomeza wengine

Hapa maneno yanayowadhuru wengine yanazungumziwa kana kwamba yalikuwa wanyama wanayo wameza watu. "maneno yanadhuru wengine"

wewe ulimu wa uongo

Hii inamaanisha mtu ambaye mwandishi anazungumza naye. "wewe msemaji wa uongo" au "wewe muongo"

atakuchukua juu ... kukunyofoa ... kukung'oa

Misemo hii yote mitatu ni njia tofauti ya kusema "kukutoa"

kukung'oa katika nchi ya walio hai

Kuwa hai duniani inazungumziwa kana kwamba watu ni mimea yenye mizizi ardhini. Mungu kumuua mtu inazungumziwa kama kuchimba mizizi ya mmea na kuitoa ardhini. "atakutoa katika nchi ya walio hai" au "Atakuua ili usiwepo tena dunia pamoja na watu waishio"

Sela

Hili linaweza kuwa neno la kimuziki linalowaongoza watu jinsi ya kuimba au kujecheza vyombo hapa. Tafsiri zingine huandika neno hili la Kiebrania, na zingine haziliweki.

Psalms 52:6

Mwenye haki pia ationa na kuogopa

"Wenye haki pia watamwona Mungu akimuondoa na watamwogopa"

Tazama

"hakika"

hakumfanya Mungu kuwa kimbilio lake

Hapa anayekimbiliwa inamaanisha mlinzi. "hakumfanya Mungu kuwa mlinzi wake" au "hakumwomba Mungu kumlinda"

Psalms 52:8

mti wa kijani wa mzeituni

Majani ya kijani ya mizeituni yana nguvu na ni imara. Hayaanguki.

mimi ni kama mti wa kijani wa mzeituni ndani ya nyumba ya Mungu

Kuwa salama inazungumziwa kama kuwa mti imara. "Nina nguvu katika nyumba ya Mungu, kama mti wa kijani wa mzeituni" au "Kwa sababu naabudu katika nyumba ya Mungu, niko salama kama mti wa kijani wa mzeituni"

ndani ya nyumba ya Mungu

Hii inamaanisha hekalu la Mungu

Nitasubiri jina lako, kwa sababu ni zuri

Jina la Mungu linamaanisha Mungu mwenyewe. Kumsubiri Mungu inaashiria kumsubiri Mungu kumsaidia. "Nitakusubiri, kwa sababu u mwema" au "Nitakusubiri unisaidie, kwa sababu u mwema"

Psalms 53

Psalms 53:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

weka katika Mahalathi

Hii inaweza kumaanisha mtindo wa muziki.

Maschili

Hii inaweza kumaanisha mtindo wa muziki.

watoto wa wanadamu

Hii inamaanisha watu wote

anayemtafuta

Kumtafuta Mungu kama mtu inazungumziwa kama "kumtafuta" Mungu. Maana zinazowezekana ni 1) kutaka kumjua Mungu. "wanaotaka kumjua yeye" au 2) kumwabudu Mungu. "wanao mwabudu yeye"

Wote wamegeuka

Kumkataa Mungu na kilicho sawa kinazungumziwa kama kugeuka. "Wote wamegeuka kutokakufanya kilicho sawa" au "Wote wamemkataa Mungu"

Psalms 53:4

Je wale wanaotenda udhalimu hawana uelewa - wale ... Mungu?

Swali hili linatumika kuonesha mshtuko ambao mwandishi anahisi kwa sababu watu wanatenda dhambi sana. Inaweza kuandikwa kama kauli mbili. "Wale wanaotenda udhalimu kana kwamba hawajui chochote. Wanawameza watu wangu kana kwamba wanakula mikate, na hawamwiti Mungu!

wale wanao wameza watu wangu kana kwamba wanakula mkate

Kuangamiza watu inazungumziwa kama kuwameza. Kufanya kana kwamba walikuwa wakila mikate inaashiria kuwa walifanya kwa urahisi sana bila kuhisi hatia. "wale wanaowaangamiza watu wangu kwa uhuru kana kwamba wanakula mikate"

Mungu ataitawanya mifupa ya yeyote atakayeweka kambi dhidi yako

Kutawanya mifupa ya watu inamaanisha kuwaua na kuruhusu mifupa yao kubaki walipofia na bila kuwazika vizuri. "Mungu atamwangamiza kabisa yeyote atakaye weka kambi dhidi yako, na mifupa yao italala imetawanyika kwenye ardhi"

yeyote atakayeweka kambi dhidi yako

Kuweka kambi dhidi ya watu inamaanisha kuwashambulia. Majeshi ya adui yalikuwa yakisafiri na kuweka kambi na kuishi kwa muda karibu na watu waliotaka kuwavamia. "yeyote atakaye wavamia"

Psalms 53:6

O, kwamba wokovu wa Israeli uje

Neno "O" hapa linatambulisha mshangao unaoonesha matumaini au ombi. "Natumaini kuwa wokovu wa Israeli utakuja" au "Ninaomba kwamba wokovu uje"

wokovu wa Israeli uje kutoka Sayuni

Wokovu unaashiria Mungu, mwokozi, ambaye hekalu lake liko Sayuni. "mwokozi wa Israeli utakuja kutoka Sayuni" au "Mungu atakuja kutoka Sayuni na kuokoa Israeli"

Mungu atakapo warudisha watu wake kutoka mateka

"Mungu atakapo okoa watu wake wafungwa"

Yakobo atasherehekea na Israeli kufurahi!

Misemo hii miwili ina maana moja.

Yakobo

Hapa "Yakobo" inamaanisha uzao wa Yakobo, Waisraeli.

Psalms 54

Psalms 54:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Taarifa ya Jumla:

Zaburi hii ni ombi kwa ajili ya msaada.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

kwenye vyombo vya nyuzi

"watu wanapaswa kucheza vyombo vya nyuzi na wimbo huu"

Maschili

Hii inaweza kumaanisha mtindo wa muziki.

Wafizi

Watu kutoka mji wa Zifu katika milima ya Yuda, kusini mashariki mwa Hebroni.

Kwani Daudi hajifichi pamoja na sisi?

Swali hili linatumika kuonesha kuwa hili ni jambo muhimu ambalo Sauli anapaswa kujua. "Daudi anajificha na sisi."

Niokoe, Mungu, kwa jina lako

Hapa jina la Mungu linaashiria tabia yake. Inaweza kumaanisha zaidi uwezo wake au haki yake. "niokoe, Mungu, kwa uwezo wako"

nihukumu katika uwezo wako

Kumhukumu Daudi hapa inaashiria kuwaonesha watu kuwa Daudi hana hatia. Mungu anapotumia nguvu zake kumwokoa Daudi, watu watajua kuwa Mungu amemhukumu na hana hatia. "Kwa uwezo wako, waoneshe watu kuwa sina hatia" au "Waoneshe watu kuwa sina hatia kwa kutumia nguvu zako kuniokoa"

yape masikio maneno ya

Kumpa mtu masikio inaashiria kumsikiliza. "sikiliza maneno yangu"

maneno ya mdomo wangu

Msemo huu unamaanisha kile alichosema mnenaji. "maneno yangu" au "ninachosema kwako"

wameinuka dhidi yangu

Kuinuka dhidi ya mtu inaashiria kujiandaa kumshambulia au kumshambulia kabisa. "wamejiandaa kunishambulia" au "wananishambulia"

watu wasio na huruma

"wanaume wasio na huruma"

wametafuta maisha yangu

Kutafuta maisha ya mtu inamaanisha kujaribu kumuua. "wamejaribu kuniua" au "wanataka kuniua"

hawajamuweka Mungu mbele yao

Kumweka Mungu mbele yao inaashiria kuwa makini na Mungu. "hawamzingatii Mungu" au "hawamjali Mungu"

Psalms 54:4

anaye nishikilia

Kumtetea Daudi na kumweka salama inazungumziwa kama kumshikilia. "anaye nitetea" au "anaye niweka salama"

Atawalipa adui zangu kwa uovu

Adhabu inazungumziwa kana kwamba ilikuwa ni malipo. "Atafanya uovu kwa adui zangu ambao walioufanya kwangu" au "Atasababisha uovu ambao adui zangu walifanya kwangu ufanywe kwao"

katika uaminifu wako, waangamize

Hapa Daudi anabadilisha kutoka kuzungumza kumhusu Mungu na kuongea naye. "Mungu, waangamize kwa sababu wewe ni mwaminifu kwangu"

Psalms 54:6

Nitatoa shukrani kwa jina lako, Yahwe, kwa kuwa ni zuri

Jina la Yahwe linamwakilisha yeye. "Nitatoa shukrani kwako, Yahwe, kwa kuwa u mwema"

jicho langu limetazama

Jicho linamaanisha mtu. "Nimetazama"

jicho langu limetazama kwa ushindi juu ya adui zangu

Maana zinazowezekana ni 1) kuona kuwa adui zake wameshindwa. "Nimeona kuwa adui zangu wameshindwa" au 2) kuwashinda adui zake. "Nimewashinda adui zangu"

Psalms 55

Psalms 55:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

kwenye vyombo vya nyuzi

"watu wanapaswa kucheza vyombo vya nyuzi na wimbo huu"

Maschili

Hii inaweza kumaanisha mtindo wa muziki.

Toa sikio kwa ombi langu

Kutoa sikio kwa mtu inamaanisha kusikiliza. "Sikiliza ombi langu"

usijifiche kwa ombi langu

Kukataa kuvutia nadhari ombi lake inazungumziwa kama kujificha mbali na hilo ombi. "usiache kujali ombi langu"

kwa sababu ya sauti ya adui zangu

Hapa "sauti" inawakilisha walichosema. "kwa sababu ya kile ambacho adui zangu wanasema"

wanaleta shida kwangu

Kusababisha taabu inazungumziwa kama kuleta taabu. "wananisababisha kuwa na taabu kubwa" au "wanafanya vitu viovu kwangu na kwa hiyo nateseka"

Psalms 55:4

Moyo wangu unatetemeka ndani yangu

Hapa, "moyo unatetemeka" inamaansiha maumivu yake ya kihisia au kuteseka. Kuteseka huku ni kwa sababu ya uoga. "Ninateseka kwa sababu ninaogopa sana"

hofu yangu ya mauti imeniangukia

Kuwa na hofu sana inazungumziwa kana kwamba hofu ni kitu kinachomwangukia mtu. "Ninaogopa sana kuwa nitakufa" au "Ninahofu kuwa nitakufa"

Uoga na kutetemeka zimeniangukia

Kuwa na hofu na kutetemeka kunazungumziwa kana kwamba hofu na kutetemeka ni vitu vinavyokuja kwa mtu. "Nimekuwa na hofu sana na kutetemeka"

kitisho kimenilemea

Kuhisi kitisho inazungumziwa kana kwamba kitisho ni kitu kinachoweza kuwafunika watu. "Ninahisi kitisho kibaya" au "Ninahofu sana"

Psalms 55:6

O, ningekuwa na mbawa kama njiwa!

Mshangao huu unaelezea kitu ambacho mwandishi anatamani sana. "Ninatamani sana ningekuwana mbawa kama njiwa"

Basi ningepaa

"Kama ningekuwa na mbawa, ningepaa"

Tazama

"Hakika"

Sela

Hili linaweza kuwa neno la kimuziki linalowaongoza watu jinsi ya kuimba au kujecheza vyombo hapa. Tafsiri zingine huandika neno hili la Kiebrania, na zingine haziliweki.

Psalms 55:8

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anamaliza kueleza alichokisema.

tufani

dhoruba kali

Wameze

Kuangamiza kitu inazungumziwa kama kukila chote. Maana zinazowezekana ni "Angamiza mipango ya adui zangu" au "Waangamize adui zangu"

changanya lugha yao

"Lugha" hapa inawakilisha kile ambacho watu walikuwa wakiambiana, na inaweza kumaanisha hasa wao kuzungumzia mipango ya kufanya uovu. Kuwachanganya inawaklisha kuwafanya watu washindwe kuelewana. "wachanganye wanapozungumza pamoja" au "changaya mipango yao"

Psalms 55:10

wanazunguka kuta zake

"vurugu na ugomzihuzunguka kuta zake." Vurugu na ugomvi zinazungumziwa kana kwamba ni watu. Hii inaweza kuelezwa kwa kuelezea watu wanaosababisha vuruguna ugomvi. "watu wanatembea kwenye kuta za mji, wakiwa na vurugu na kupigana"

kuta zake

"juu ya kuta za mji" Miji ilikuwa imezungukwa na kuta nene za kuwalinda na adui. Watu waliweza kutembea juu ya kuta kuona kama kuna adui wanaokuja kwenye mji.

udhalimu na shida ziko katikati yake

Udhalimu na shida zinazungumziwa kana kwamba ni watu. "watu hufanya udhalimu na kuleta shida.katikati ya mji" au "watu hufanya matendo ya dhambi na kusababisha shida ndani yake"

shida

"taabu"

Uovu uko katikati yake

Uovu unazungumziwa kana kwamba ni mtu. "Watu hufanya vitendo vya uovu katikati ya mji" au "watu huteketeza vitu katika mji"

dhuluma na uongo haziondoki mitaa yake

Dhuluma na uongo zinazungumziwa kana kwamba ni watu. "Watu hudhulumu na kuwadanganya wengine katika mitaa ya mji, na hawaondoki" au "Watu huwadhulumu na kuwadanganya wengine katika mitaa ya mji"

mitaa yake

Hii inaweza kumaanisha sehemu za masoko katika mji.

Psalms 55:12

ningeweza kuibeba

Kuvumilia kukemewa inazungumziwa kama kuubeba. "ningeweza kubeba kukemewa" au "nisingekuwa na huzuni sana kuhusu kukemewa"

aliyejiinua dhidi yangu

Kuwa na majivuno na kumtusi mwingine inazungumziwa kama kujiinua dhidi ya mwingine. "kanitukana mimi" au "kanichukia"

Lakini ilikuwa ni wewe

Mwandishi wa zaburi anazungumza kana kwamba mtu aliyemkemea na kumsuta alikuwa hapo akimsikiliza.

mwenzangu na rafiki wangu wa karibu

"Wewe ulikuwa mwenzangu na rafiki wa karibu"

Sisi

Neno "sisi" inamaanisha mwandishi wa zaburi na rafiki yake.

pamoja na umati

Maana zinazowezekan ni 1) "pamoja" au 2) "pamoja na kundi"

Psalms 55:15

Acha mauti ije kwao ghafla

Mauti inazungumziwa kana kwamba ni mtu anayeweza kushambulia watu. "Acha adui zangu wafe ghafla"

acha waende chini kuzimu wakiwa hai

Kufa ghafla inazungumziwa kana kwamba watu walitakiwa kwenda kuzimu haraka sana hadi hawakufa kwanza. "acha waende kuzimu ghafla'

uovu ndipo wanapoishi

Uovu unazungumziwa kana kwamba ni kitu kinachoweza kuwa sehemu fulani. Tabia ya uovu ya adui zake inazungumziwa kana kwamba uovu ulikuwa pamoja nao au akribu yao. "huwa wanafanya vitu viovu wanapoishi"

katikati yao

Msemo huu unawekea mkazo wazo la uovu kuwa karibu yao sana. Hapa uovu unazungumziwa kama kutokuwa tu kwenyenyumba zao, bali mahali walipo. "Huwa wanafanya vitu viovu popote walipo" au "popote walipo"

Psalms 55:16

Mimi

Msemo huu unaonesha kuwa mwandishi ameacha kuzungumzia kitu kimoja na sasa ameanza kujizungumzia mwenyewe.

kuguna

"kulia"

atasikia sauti yangu

Hapa "sauti" inawakilisha kati ya 1) mwandishi wa zaburi au 2) malalamiko ya mwandishi wa zaburi au kilio chake. "atanisikia" au "atasikia kuguna kwangu"

maisha yangu

Hapa "maisha" inamwakilisha mwandishi wa zaburi. "mimi"

kwa kuwa wale waliokuwa wakipigana dhidi yangu walikuwa wengi

"kwa kuwa watu wengi walipigana dhidi yangu"

Psalms 55:19

atawasikia

"atawasikia adui zangu" au "atasikia kile ambacho adui zangu wanasema." Tafsiri zingine zinasema "watanisikia."

kuwaaibisha

"atawashinda na kuwaaibisha"

Psalms 55:20

ameinua mikono yake dhidi ya wale

Kuinua mkono dhidi ya watu inawakilisha kuwashambulia. Hii inaweza kuwa sitiari ya kusema vitu vinavyowaweka watu katika hatari au kuwasababisha kuwa katika shida. "amewashambulia wale" au "amewasiliti wale"

Mdomo wake

"Mdomo" wa mtu unawakilisha anachosema. "Kile ambacho rafiki yangu amesema"

Mdomo wake ulikuwa laini kama siagi

Maneno yanayopendeza au mazuri kusikia yanazungumziwa kana kwamba ni malaini na mepesi kumeza. "Alichosema kinapendeza kama siagi laini" au "Alisema vitu vizuri"

uhasama

"ovyo" au "chuki"

maneno yake

"Maneno" ya mtu yanawakilisha anachosema. "Alichosema"

maneno yake yalikuwa laini kuliko mafuta

Watu huweka mafuta kwenye ngozi zao kuifanya ijisikie vizuri, na huweka kwenye vidonda kuviponya. Maneno yaliyo yenye huruma au yenye msaada yanazungumziwa kana kwamba yalikuwa laini au ya kumbembeleza. "aliyosema yalikuwa yenye huruma na ya kumbembeleza kama mafuta" au "alisema vitu venye huruma"

yalikuwa panga zilizo chomolewa

Maneno yanayosababisha shida kwa watu yanazungumziwa kana kwamba ni panga zinazoweza kuumiza watu. "kile alichosema kiliwaumiza watu kama panga zilizochomolewa zifanyavyo" au "alichosema kiliwasababishia watu shida"

panga zilizo chomolewa

Neno "chomolewa" hapa linamaanisha kuwa panga zimetolewa kwenye makasha yake tayari kwa kutumiwa.

Psalms 55:22

Weka mizigo yako

Hapa mwandishi anazungumza na watu wanyofu wengine.

Weka mizigo yako kwa Yahwe

Hapa taabu zinazungumziwa kana kwamba ni mizigo ambayo watu wanatakiwa kubeba. Kumtumaini Mungu kutusaidia wakati tuna shida inazungumziwa kama kumwekea mizigo yetu juu yake ili atubebee. "Mpe Yahwe shida zako" au "Mwamini Yahwe kukusaidia na taabu zako zote kama mtu anavyomwamini mtu mwenye nguvu zaidi kubeba mzigo wake"

atakuchukua

Kumtunza mtu au kumsaidia mtu akiwa na shida inazungumziwa kama kumsaidia. "atakutunza" au "atakulinda"

kamwe hataruhusu mtu mwenye haki kupepesuka

Mtu ambaye anataka kudhuriwa vibaya na maafa fulani inazungumziwa kana kwamba anapepesuka au kuyumba na anataka kuanguka. "hatamuacha mtu mwenye haki ayumbe na kuanguka" au "hataacha mtu mwenye haki aangamizwe"

Lakini wewe, Mungu

Mwandishi anazungumza na Yahwe sasa.

shimo la uharibifu

Hii inaweza kumaanisha kaburi au jahannamu.

utawaleta waovu chini kwenye shimo la uharibifu

Hii inawakilisha kuwasababisha watu kufa. "utawasababisha waovu wafe" au "utawasababisha watu waovu kufa na kwenda sehemu ambapo wafu wapo"

wenye kiu ya damu na watu waongo

"watu wanadanganya na wanaotaka kuwaua wengine" au "wauaji waongo"

hata nusu ya urefu wa wengine

hata nusu ya urefu wa uhai wa wengine

Psalms 56

Psalms 56:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

weka katika Yothani elemu rehokimu

Hii inaweza kuwa inaeleza mtindo au tuni ya muziki ya kutumia wakati wa kuimba zaburi hii. "Imba zaburi hii kwa kutumia tuni ya "Yothani elemu rehokimu" au "Imba kwa kutumia mtindo wa Yothani elemu rehokimu"

Yothani elemu rehokimu

Hii inaweza kumaanisha "Njiwa katika Miti ya Mwaloni ya Mbali."

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Michtamu

Maana ya neno "michtamu" haieleweki. Hii inaweza kuandikwa kama: "Hii ni zaburi ambayo Daudi aliandika."

wakati Wafilisti walipomchukua Gathi

"Wafilisti walipomkamata Gathi"

wanakandamiza shambulio lao

"wanakuja karibu na karibu ili kunishambulia"

Adui zangu wananikanyaga

Shambulio kali la adui linazungumziwa kana kwamba walikuwa wakitumia mwili wake kutembea. "Adui zangu wananishambulia sana"

Psalms 56:3

kwako

Neno "kwako" linamaanisha Mungu.

mtu tu anaweza kufanya nini kwangu?

Hapa swali linatumika kuonesha kuwa mwandishi wa zaburi haogopi watu, kwa sababu hawawezi kumdhuru kabisa. "watu tu hawawezi kufanya kitu kwangu!" au "watu tu hawawezi kunidhuru vibaya!"

mtu tu

"watu." Hii inadokezwa kuwa watu hawana nguvu, lakini Mungu ana uwezo.

Psalms 56:5

Siku nzima

"wakati wote"

wanapindisha maneno yangu

Kurudia kile ambacho mtu amesema lakini kubadilisha kidogo ili imaanishe kitu tofauti inazungumziwa kama kupindisha maneno yao. "wanasema kuwa nimesema vitu ambavyo sijasema" au "wanadai kuwa nimesema vitu, lakini wanadanganya"

mawazo yao yote yako dhidi yangu kwa uovu

"daima huwa wanan mawazo maovu dhidi yangu" au "daima huwa wanawaza mambo maovu ya kunifanyia"

wanaangalia hatua zangu

Kuangalia kile ambacho mtu anafnya ili kuona jinsi ya kumsababishia shida inazungumziwa kama kuangalia hatua zake, kama mtu anavyotaka kumkamata mtu anavyoangalia mtu anapotembea. "wanaangalia kila kitu nachofnaya"

kama tu walivyo subiri kwa ajili ya maisha yangu

Kusubiri kumua mtu inazungumziwa kama kusubiri maisha yake. "wanaposubiri kuniua"

Psalms 56:7

Usiache watoroke kufanya udhalimu

"Usiwaache watoroke adhabu yako kwa ajili ya udhalimu wao" au "Usiwaache watoroke unapowaadhibu kwa mambo maovu wanayofanya"

Uwalete chini watu

Kuwashinda adui inazungumziwa kama kuwaleta chini. "Washinde watu"

Unahesabu kuzurura kwangu

Kujishughulisha kwa Mungu juu ya mwandishi wa zaburi inazungumziwa kana kwamba Mungu alihesabu kila wakati ambao mwandishi wa zaburi alite

na kuweka machozi yangu kwenye chupa yako

Kujishughulisha kwa Mungu juu ya mwandishi wa zaburi inazungumziwa kana kwamba Mungu alitunza machozi ya mwandishi wa zaburi kwenye chupa. Machozi yanawakilisha kulia. "na unajua jinsi nilivyolia na unanijali"

hazimo kwenye kitabu chako?

Kujishughulisha kwa Mungu juu ya mwandishi wa zaburi inazungumziwa kana kwamba aliandika idadi ya machozi ya mwandishi wa zaburi katika kitabu chake. Swali hili linatumika kumkumbusha Mungu jinsi anavyomjali sana mwandishi. "umeandika kuyahusu katika kitabu chako" au "unakumbuka machozi yangu"

Psalms 56:9

watageuka

"watakimbia" au "watageuka na kukimbia"

Mungu yu upande wangu

Hii inamaanisha kuwa Mungu anamwonesha fadhila. Katika hali hii inadokezwa kuwa Mungu anapambana dhidi ya adui wa mwandishi wa zaburi ili kumlinda. "Mungu ananipigania"

Yeyote anaweza kunifanya nini?

Swali linatumika hapa kuonesha kuwa mwandishi wa zaburi haogopi watu, kwa sababu hawawezi kumuumiza sana. "Watu hawawezi kunifanya kitu!" au "Watu hawawezi kuniumiza vibaya!"

Psalms 56:12

Jukumu la kutimiza nadhiri zangu kwako liko juu yangu

Kuwajibika kufanya kitu inazungumziwa kana kwamba jukumu lakufanya kitu liko juu yamtu. "Lazima nitimize nadhiri zangu kwako" au "Lazima nifanye nilichoahidi kwako kufanya"

umiitunza miguu yangu na kuanguka

Hapa miguu inamwakilisha mtu. Kuanguka hapa inaweza kuwakilisha kuuwawa na adui zake. "umenepusha na kuanguka" au "umeniepusha na kuuwawa na adui zangu"

ili kwamba nitembee mbele za Mungu

Kuishi na kuonwa na Mungu inazungumziwa kama kutembea mbele ya Mungu. "ili kwamba niishi mbele ya uwepo wa Mungu"

katika nuru ya walio hai

Hapa "nuru ya walio hai" inaweza kuwa inawakilisha Mungu kuwawezesha watu kuishi. "na uhai unaotoa" au "kwa sababu unaniwezesha kuishi"

Psalms 57

Psalms 57:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

weka katika Al Tashhethi

Hii inawezakuwa inaeleza mtindo wa muziki au tuni ya kutumia wakati wa kuimba zaburi hii. "imba zaburi hii kwa kutumia tuni ya 'Al Tashhethi'" au

Al Tashhethi

Hii inamaanisha "Usiangamize."

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Michtamu

Maana ya neno "michtamu" haiko wazi. Hii inaweza kuandikwa kama: "Hii ni zaburi aliyoandika Daudi."

alipotoroka kutoka kwa Sauli, katika pango

"Hii ina husu Daudi alipojificha kwenye pango akimkimbia Sauli" au "Hii ina husu wakati mfalme Sauli alipokuwa anamfukuza Daudi, na Daudi akajificha kwenye pango"

ninakukimbilia

Kwenda kwa Yahwe kwa ajili ya ulinzi inazungumziwa kama kumkimbilia. "ninaenda kwako kwa ajili ya ulinzi"

ninakaa chini ya mbawa zako kwa ajili ya ulinzi

Mwandishi anamzungumzia Mungu kana kwamba ni ndege anayelinda makinda yake kwa kuwaficha chini ya mbawa zake. "nakuamini wewe kunilinda"

hadi uharibifu wake uishe

Mwandishi wa zaburi anazungumzia hamu ya Sauli kumuua kana kwamba Sauli alikuwa akitafuta kumwangamiza adui. "hadi shida hii iishe" au "hadi nitakapo kuwa siko hatarini tena"

Psalms 57:2

anayefanya vitu hivi vyote kwa ajili yangu

Hii inaeleza kwa nini atalia kwa Mungu. "kwa sababu hufanya vitu vyote kwa ajili yangu"

wale wanao niponda

Mashambulizi makali ya adui yanazungumziwa kana kwamba yalikuwa wakikandamiza mwili wake kwa kutembea juu yake. "wale wanaonishambulia kwa ukali"

Mungu atanitumia upendo wake wa huruma na uaminifu wake

Huruma na uaminifu wa Mungu unazungumziwa kana kwamba anatuma huruma yake na uaminifu wake. "Mungu atakuwa na huruma kwangu na mwaminifu"

Psalms 57:4

Maisha yangu yako katikati ya simba

Mwandishi anazungumzia adui zake kana kwamba ni simba. "Ninaishi katikati ya adui wakali" au "Adui wakali wananizunguka kama simba"

wale walio tayari kunimeza

Kuangamiza inazungumziwa kama kumeza au kula kitu. Tafsiri zingine zinaelewa neno la Kihebrania kumaanisha "wanyam wa moto." Picha zote zinazungumzia adui zake kana kwamba ni wanyama pori. "wale walio tayari kuniangamiza"

watu ambao meno yao ni mikuki na mishale

Mikuki na mishale ya wanyama inazungumziwa kana kwamba ni meno ya simba. Mwandishi wa zaburi anaendelea kuzungumzia adui zake kana kwamba ni simba. "watu wanaowaua wengine kwa mikuki na mishale kama simba wanavyoua kwa meno yao makali"

mikuki na mishale

Hizi ni silaha za vita.

ambao ndimi zao ni panga kali

Ulimi unawakilisha kile ambacho mtu anasemam na maneno mabaya ya adui yanazungumziwa kana kwamba ni panga. "ambao maneno yao ni kama panga kali" au "wanaosababisha taabu kubwa kwangu kwa sababu ya kile wanachosema"

Uinuliwe, Mungu, juu ya mbingu

Mwandishi anamwomba Mungu kuonesha kuwa ameinuliwa. Kuinuliwa juu ya mbingu inawakilisha kuwa mkuu. "Mungu, onesha kuwa umeinuliwa juu ya mbingu" au "Mungu, onesha kuwa wewe ni mkuu katika mbingu"

acha utukufu wako uwe juu ya dunia

Mwandishi wa zaburi anamwomba Mungu kuonesha utukufu wake. "onesha utukufu wako duniani kote"

Psalms 57:6

Wanasambaza wavu kwa ajili ya miguu yangu

Mipango ya adui zake kumshika inazungumziwa kana kwamba walisambaza wavu kwenye ardhi ili kumnasa. "Ni kana kwamba adui zangu wamesambaza wavu kwa ajili ya kuninasa" au "Walipanga kunishika kama watu wanavyosambaza wavu kumnasa mnyama"

Walichimba shimo mbele yangu

Mipango ya adui zake kumshika inazungumziwa kana kwamba walichimba shimo kwa ajili yake kuangukia. "Ni kana kwamba walichimba shimo kwa ajili yangu kuangukia" au "Walipanga kunishika kama watu wanaochimba shimo kwenye ardhi kumnasa mnyama"

Wao wenyewe wameanguka katikati yake

Madhara yaliyokuja kwa adui zake walivyojaribu kumnasa inazungumziwa kana kwamba walianguka kwenye mtego walioandaa kwa ajili yake. "Wao wenyewe walianguka katika shimo walilochimba kwa ajili yangu" au "Lakini wao wenyewe waliumizwa kwa kile walichojaribu kufanya kwangu"

Psalms 57:7

Moyo wangu ni thabiti, Mungu, moyo wangu ni thabiti

Kuwa jasiri inazungumziwa kama moyo wa mtu kuwa imara badala ya kutikiswa au kusogezwa kirahisi. Msemo huu unarudiwa kuonesha kuwa ana imani kamili kwa Mungu na hata badilika. "Nina imani kamili kwako, Mungu"

Nitaimba sifa

"Mimi nitaimba sifa kwako, Mungu"

Amka, moyo wangu ulio heshimiwa

Kuamka inaweza kuwa sitiari ya kuanza au kujiandaa kufanya kitu. Moyo unamwakilisha mwandishi wa zaburi au hisia zake. "Amka, moyo wangu ulio heshimiwa, imba sifa kwa Mungu" au "Nina heshima kuamka na kuimba sifa kwa Mungu"

amka, kinanda na kinubi

Mwandishi anazungumza kana kwamba kinanda na kinubi ni watu wanaoweza kuimba sifa kwa Mungu. "Amka, kinanda na kinubu na imbeni sifa kwa Mungu" au "Nitacheza kinanda na kinubi huku ninaimba sifa kwa Mungu"

Nitauamsha alfajiri

Alfajiri inazungumziwa kana kwamba iko hai, na kuamka kabla ya alfajiri inazungumziwa kama kuuamsha. Lengo la kuamka kabla ya alfajiri ni kumsifu Mungu. "Nitaamka kabla ya alfajiri" au "Nitaamka kabla jua halijachomoza"

Psalms 57:9

Kwa kuwa upendo wako usio koma ni mkuu, unafika mbinguni ... uaminifu wako hadi mawinguni

Misemo hii miwili inamaana ya kukaribiana. Ukuu wa upendo wa Mungu usio koma na ukuu wa uaminifu wake zinazungumziwa kana kwamba zinaweza kupimwa kwa umbali.

Kwa kuwa upendo wako usio shindwa ni mkuu, unafika mbinguni

Ukku wa upendo usio shindwa wa Mungu unazungumziwa kana kwamba unaweza kupimwa kwa umbali. "Upendo wako usio shindwa ni mkuu kama umbali wa kutoka duniani hadi mbinguni"

na uaminifu wako hadi mawinguni

"na uamonifu wako ni mkuu, unafika mawinguni" au "na uaminifu wako ni mkuu kama umbali wa kutoka duniani hadi mawinguni"

Utukuzwe, Mungu, juu ya mbingu

Mwandishi anamwomba Mungu kuonesha kuwa ameinuliwa. Kuinuliwa juu ya mbingu inawakilisha kuwa mkuu. "Mungu, onesha kuwa umeinuliwa juu ya mbingu" au "Mungu, onesha kuwa wewe ni mkuu katika mbingu"

utukufu wako uinuliwe juu ya dunia wote

Mwandishi wa zaburi anamwomba Mungu kuonesha utukufu wake. "onesha utukufu wako juu ya dunia yote"

Psalms 58

Psalms 58:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Taarifa ya Jumla:

Zaburi hii ni wimbo kuhusu watu waovu.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

weka katika Al Tashhethi

Hii inaweza kuwa inaeleza mtindo wa muziki au tuni ya kutumia wakati wa kuimba zaburi hii.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Michtamu

Maana ya neno "Michtamu" haiko wazi. Hii inaweza kuandikwa kama: "Hii ni zaburi ambayo Daudi aliandika"

Je, watawala wenu wanazungumza haki?

Mwandishi anatumia swali hili kukemea watawala kwa sababu hawazungumzi kwa haki. "Nyie watawala hamsemi kilicho haki!"

nyie ... mwenu

Hapa wanaozungumziwa ni watu wenye nguvu ambao ni waamuzi.

Huwa mnahukumu kwa unyofu, nyie watu?

Mwandishi anatumia swali hili kukemea waamuzi ambao awahukumu kwa unyofu. "Nyie watu huwa hamhukumu watu kwa unyofu!"

Hapana

Mwandishi anajibu maswali mawili aliyouliza.

unatenda uovu katika moyo wako

Moyo unawakilisha mawazo au mipango ya watu. "mnatenda uovu katika mawazo yenu" au "mnawaza kuhusu kufanya vitu viovu"

unasamba vurugu katika nchi nzima kwa mikono yako

Kufanya vurugu katika sehemu mbali mbali katika nchi inazungumziwa kama kusambaza vurugu kwenye nchi, kana kwamba vurugu ni aina fulani ya kitu. "nyie wenyewe huwa mnafanya matendo ya vurugu kila sehemu katika nchi"

Psalms 58:3

Waovu wanapotoka hata walipokuwa tumboni ... wanaenda pembeni tangu kuzaliwa

Hili ni wazo moja linaloelezwa kwa njia mbili tofauti.

wanapotoka

Kufanya vitu vibaya inazungumziwa kana kwamba watu wanatembea kwenye barabara, na wanageuka na kukosea njia. "wanafanya makosa"

Sumu yao ni kama sumu ya nyoka

Vitu viovu ambavyo watu wanasema vinazungumziwa kana kwamba ni sumu. "Maneno yao maovu yanasababisha shida kama sumu ya nyoka inavyowadhuru watu"

ni kama fira kiziwi anayezuia maskio yake

watu waovu wasiosikia ushauri au kukemewa wanazungumziwa kana kwamba ni nyoka ambazo haziitikii muziki wa mganga. "wanakataa kusikiliza kama fira kiziwi inayozuia maskio yake"

fira kiziwi anayezuia maskio yake

Fira asiyeitikia muziki wa mganga anazungumziwa kana kwamba inaweza kuweka kitu katika maskio yake ili kwamba isisikie. "fira asiye sikia"

fira

aina ya nyoka mwenye sumu

waganga

watu wanaocheza au kuimba muziki ili kumwongoza nyoka

haijalishi ujuzi wao ulivyo

"haijalishi ujuzi walionao waganga katika kumwongoza nyoka"

Psalms 58:6

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaendelea kuorodhesha vitu ambavyo anapenda Mungu awafanyie watu waovu.

Vunja meno yao ... vunja nje meno makuu ya simba wachanga

Katika misemo hii miwili, watu waovu wanazungumziwa kana kwamba ni simba, na kuwafanya wanyonge kuua watu inazungumziwa kama kuvunja meno yao. "Chukua nguvu yao ya kuua. Uwafanye kuwa wanyonge kama simba wachanga ambao meno yao yamevunjwa na kuanguka nje"

Acha wayeyuke kama maji yanayotiririka

Watu waovu wanazungumziwa kana kwamba ni barafu au maji. Kutokuwepo tena inazungumziwa kama kuyeyuka au maji kutiririka kwenye ardhi kavu. "Wafanye wapotee kama maji yanayotiririka" au "Wafanye wapotee kama barafu inayoyeyuka na kutiririka kwenye ardhi"

acha wawe kana kwamba hawana ncha

"acha mishale yao iwe kama haina ncha"

Acha wawe kama konokono inayoyeyuka na kupita

Kutokuwepo tena inazungumziwa kama kuyeyuka na kupotea. "Acha waovu wapotee kama konokono anayeyuka na kutokuwepo tena"

konokono

"koa"

kama mtoto wa mwanamke aliyezaliwa kabla ya muda ambaye hajaliona jua

Kutokuwepo kunazungumziwa kama kuwa kama mtoto anayezaliwa akiwa amekufa. "kama mtoto anayezaliwa mapema sana kuishi na kuona mwanga wa jua" au "kama mtoto alizaliwa akiwa amekufa"

Psalms 58:9

Kabla masufuria yenu hayajajaza moto wa kuchoma wa miiba ... miiba ya kijana na miiba ya kuchoma pamoja

Waovu wanazungumziwa kana kwamba walikuwa matawi ya miti ya miiba, na hukumu ya haraka ya Mungu juu yao inazungumziwa kana kwamba atawapuliza au kuwafagia haraka. "Mungu atawaangamiza watu waovu haraka zaidi ya kimbunga kinavyoweza kupuliza matawi ya miiba yaliyowekwa chini ya sufuria la kupikia na kuchomwa na moto"

yenu

Daudi anazungumza na watu wa Mungu.

mwiba

"matawi ya miiba"

Mwenye haki atafurahi atakapoona

Msemo "mwenye haki" inamaanisha watu wenye haki kwa ujumla. "Watu wenye haki watafurahi watakapoona"

ataosha miguu yake kwenye damu ya waovu

Kuloanisha miguu ya mtu kwa kutembea kwenye damu inazungumziwa kama kuosha miguu katika damu. "wenye haki wataloanisha miguu yao katika damu ya waovu" au "wenye haki watatembea katika damu ya waovu"

ataosha miguu yake kwenye damu ya waovu

Idadi kubwa ya watu waovu wanaokufa inaelezwa kwa kutumia kukuza kwa neno la watu wenye haki kuosha miguu yao katika damu ya watu waovu. "watu wengi sana waovu watakufa hadi wenye haki watakapotembea kwenye damu yao, itaonekana kana kwamba wanaweza kuosha miguu yao humo"

Psalms 59

Psalms 59:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

weka katika Al Tashhethi

Hii inaweza kuwa inaeleza mtindo wa muziki au tuni ya kutumia wakati wa kuimba zaburi hii.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Michtamu

Maana ya neno "michtamu" haiko wazi. Hii inaweza kuandikwa kama: "Hii ni zaburi ambayo Daudi aliandika"

Sauli alipotuma, na wakaangalia nyumba kumuua

"katika kipindi Sauli alipowatuma askari wake kwenda na kuangalia nyumba ya Daudi kwa ajili ya nafasi ya kumuua"

niweke juu

Sehemu ya juu inawakilisha sehemu salama ambapo adui zake hawawezi kumfikia. "niweke sehemu salama"

inuka dhidi yangu

Kuinuka dhidi ya mtu inawakilisha kumshambulia. "wananishambulia"

watu wenye kiu ya damu

""watu wenye hamu ya kuua" au "watu wanaopenda kuua watu"

Psalms 59:3

wanasubiri kunivamia ili kuchukua uhai wangu

Adui wa Daudi wako katika maficho na wanasubiri kwa utulivu kwa muda ambao watamvamia.

amka

Kuamua kufanya kitu na kuanza kukifanya inazungumziwa kama kuamka. "fanya kitu" au "chukua hatua"

na uone

"na tazama kinachotokea kwangu" au "na uone wanachonifanyie mimi"

Psalms 59:5

inuka

Kuamua kufanya kitu na kuanza kukifanya inazungumziwa kama kuamka. "fanya kitu" au "chukua hatua"

mataifa yote

Neno "mataifa" hapa yanawakilisha watu wa mataifa ambao hawamtukuzi Mungu. "watu wa mataifa yote"

Psalms 59:6

Wanarudi jioni

Wanaorudi ni watenda maovu.

wanalia kama mbwa

Mwandishi anazungumzia vitishio vya adui zake kushambulia watu kana kwamba walikuwa ni mbwa wanaolia, kunguruma, au kubweka kwa watu. "wanatishia kushambulia watu"

kuuzunguka mji

"kuuzunguka mji kumshambulia yeyote watakayemkuta"

Tazama

Hapa neno "Tazama" linatumika kuvuta nadhari kwa kitu. "Sikia"

wanateuka kwa midomo yao

Kusema vitu viovu inazungumziwa kama kuteuka. Vitu hivi vibaya vinaweza kuwa ni matusi au vitisho. "wanasema vitu vibaya" au "wanapiga kelele kwa kusema vitu vibaya"

teuka

kutoa pumzi kwa nguvu kutoka mdomoni; kuruhusu hewa kutoka tumboni kupitia mdomoni kwa sauti kubwa ya kuudhi.

panga ziko kwenye midomo yao

Vitu vya ukatili ambavyo watu waovu walikuwa wakisema vinazungumziwa kana kwamba ni panga. "wanasema vitu vya ukatili vinavyosababisha watu taabu kama panga zinavyoangamiza watu"

Nani anatusikia?

Swali hili linatumika kuonesha kuwa waliamini kuwa Mungu hatawasikia na kuwaadhibu. "Hakuna mtu anayetusikia!" au "Mungu wenu hatusikii!"

Psalms 59:8

wachekee

"wachekee kwa dharau" au "wadhihaka." Mungu aliwachekea kwa sababu walikuwa hawafai na dhaifu.

unashilia mataifa yote katika dhihaka

"unafanyia mzaha mataifa yote" au "unajua kuwa watu wa mataifa ni wapumbavu"

dhihaka

"fanyia mzaha" au "kejeli"

nguvu yangu

Mungu kuwa nguvu ya mwandishi wa zaburi inawakilisha Mungu kumlinda. "wewe ni nguvu yangu" au "wewe ni mlinzi wangu"

wewe ni mnara wangu wa juu

Mnara wa juu ni sehemu ambapo watu wanaweza kwenda kwa ajili ya kivuli kutoka kwa adui zao. Mwandishi wa zaburi anamzungumzia Mungu kumlinda kana kwamba Mungu ni kivuli imara na salama. "unanilinda kama mnara wa juu"

Psalms 59:10

Mungu wangu atakuna na mimi

Mungu kumwokoa mwandishi wa zaburi inazungumziwa kana kwamba Mungu alikuwa anatakiwa kukutana naye. "Mungu wangu ataniokoa"

hamu yangu kwa adui zangu

"nachotaka kitokee kwa adui zangu"

Watawanye

"Wasababishe wazurure"

ngao yetu

Mungu kumlinda mwenye haki inazungumziwa kana kwamba Mungu ni ngao. "mlinzi wetu" au "yule anyetulinda kama ngao"

Psalms 59:12

Kwa dhambi za midomo yao na maneno ya midomo yao

Midomo inawakilisha vitu ambavyo watu husema. "Kwa sababu wanatenda dhambi kwa kile wanachokisema" au "Kwa sababu ya maneno ya dhambi wanayoyasema"

acha wakamatwe katika kiburi chao

"acha watu wawashike kwa sababu ya kiburi chao"

wanayoonesha

"wanayosema"

Wameze katika gadhabu yako, wameze ili wasiwepo tena

Kuwaangamiza kabisa inazungumziwa aidha kati ya kuwachoma au kuwala. "Kuwa na hasira nao na waangamize kabisa ili wasiwepo tena"

katika Yakobo

Yakobo hapa inamaanisha Israeli. "katika Israeli"

hadi mwisho wa dunia

"hadi sehemu za mbali zaidi duniani." Hii inawakilisha sehemu zote duniani. "sehemu zote duniani"

Psalms 59:14

kulia kama mbwa

Mwandishi anazungumzia adui zake kutishia kushambulia watu kana kwamba ni mbwa wanalia, wanaunguruma, au wanawabwekea watu. "wanatishia kutushambulia" au "wanatishia kutushambulia kama mbwa pori"

ridhika

"tosheki"

Psalms 59:16

umekuwa mnara wangu wa juu na kimbilio langu

Minara ya juu na sehemu za kukimbilia ni mahali ambapo watu wanaweza kwenda kwa ajili ya kivuli kutoka kwa adui zao. Mwandishi anazungumzia Mungu kumlinda kana kwamba Mungu alikuwa kivuli imara na salama. "umenilinda kama mnara wa juu na kimbilio.

katika siku ya dhiki yangu

"Neno "siku" hapa inamaanisha kipindi katika wakati. "wakati nina taabu"

Kwako, nguvu yangu, nitaimba sifa

"Wewe ni nguvu yangu, kwa hiyo nitaimba sifa kwako"

nguvu yangu

Mungu kuwa nguvu ya mwandishi wa zaburi inazungumziwa kama Mungu kumlinda. "mlinzi wangu"

kwa Mungu ni mnara wangu wa juu

Minara ya juu na sehemu za kukimbilia ni mahali ambapo watu wanaweza kwenda kwa ajili ya kivuli kutoka kwa adui zao. Mwandishi anazungumzia Mungu kumlinda kana kwamba Mungu alikuwa kivuli imara na salama. "umenilinda kama mnara wa juu na kimbilio.

Mungu wa agano la umanifu

Hii inaweza kuelezwa katika sentensi tofauti. "Yeye ni Mungu wa agano la uaminifu" au "Wewe ni Mungu wa agano la uaminifu"

Psalms 60

Psalms 60:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

weka katika Shushani Eduthi

Hii inaweza kuwa inaeleza tuni au mtindo wa muziki wa kutumia wakati wa kuimba zaburi hii. "imba zaburi hii kwa kutumia tuni ya 'Shushani Eduthi'" au "imba hii kwa kutumia mtindo wa Shushani Eduthi"

Shushani Eduthi

Hii inamaanisha "Yungiyungi ya Ahadi"

Michtam

Maana ya neno "michtamu" haliko wazi. Hii inaweza kuandikwa kama: "Hii ni zaburi ambayo Daudi aliandika"

Aramu Naharaimu ... Aramu Soba

"Aramu wa mito miwili ... taifa la Aramu la Soba." Hizi ni sehemu.

Yoabu

Hii inamaanisha Yoabu na jeshi aliloongoza.

watu elfu kumi na mbili wa Edomu

watu wa Edomu 12,000"

umetutupa

Mungu kuwakataa watu inazungumziwa kana kwamba amewatupa. "umetukataa"

umevunja kwenye ulinzi wetu

Mungu kuwaruhusu adui wa Israeli kuvunja kwenye ulinzi wao inazungmziwa kama Mungu mwenyewe amefanya hivyo. "umewaruhusu adui zetu kuvunja kwenye ulinzi wetu"

Psalms 60:2

Kauli Unganishi:

Mwandishi wa zaburi anaendelea kuzungumza na Mungu.

Umeifanya nchi kutetemeka; umeichana

Mwandishi wa zaburi anazungumzia maafa katika nchi yake kana kwamba ni tetemeko.

ponya nyufa zake

Kuwafanya watu kuwa na nguvu tena inazungumziwa kama kurekebisha nyufa chini na kwenye kuta.

nyufa

upenyo mkubwa chini au kwenye kuta

Umewafanya watu wako waone vitu vigumu

Hapa "tazama" inawakilisha "kupitia" au "kuteseka"

kunywa divai ya kupepesuka

"divai inayotufanya tupepesuke." Kutojiweza inazungumziwa kama kupepesuka, kushindwa kusima wima vizuri.

Psalms 60:4

umeweka benderea

Mungu kuwaongoza watu wake vitani inazungumziwa kana kwamba Mungu ni binadamu mfalme au kamanda mkuu aliyeweka bendera kwa ajili ya jeshi lake. "wewe ni kama mfalme anayeweka bendera" au "unatuagiza vitani kama mfalme anayeinua bendera"

bendera

"bendera ya vita." Hii ni bendera ambayo mfalme au kamanda huinua kwenye nguzo kuonesha kuwa jeshi linapaswa kukusanyika.

kuonesha dhidi ya wale waliobeba upinde

"kuonesha dhidi ya wale waliobeba upinde."

kuonesha dhidi ya wale waliobeba upinde

Msemo huu "wale waliobeba upinde" unamaanisha jeshi la adui vitani. "kuonesha wakati akipeleka jeshi lake vitani dhidi ya adui zako"

kwa mkono wako wa kuume

Mkono wa kuume wa Mungu unaashiria nguvu. "kwa nguvu yako"

nijibu

Kumjibu hapa inawakilisha kuitikia ombi lake. "itikiaombi langu" au "jibu ombi langu"

Psalms 60:6

Efraimu pia ni kofia yangu ya chuma

Mungu anazungumzia kabila la Efraimu kana kwamba ni jeshi lake. Kofia inaashiria kifaa cha vita. "Efraimu ni kama kofia yangu ya chuma niliyochagua" au "kabila la Efraimu ni jeshi langu"

kofia ya chuma

kofi ngumu ambayo askari huvaa kulinda kichwa chake dhidi ya ajali

Yuda ni fimbo yangu

Mungu alichagua wanaume kutoka kabila la Yuda kuwa wafalme wa watu wake, na anazungumzia kabila hilo kana kwamba ni fimbo yake. "kabila la Yuda ni kama fimbo yangu" au "Yuda ni kabila ambalo natawalia watu wangu"

Psalms 60:8

Moabu ni bakuli langu la kunawia

Mungu anazungumzia Moabu kutokuwa muhimu kana kwamba Moabu ni bakuli la kunawia au mtumishi wa chini. "Moabu ni kama bakuli nilalotumia kunawia"

juu ya Edomu nitarusha kiatu changu

Inawezekana Mungu alikuwa akizungumzia kuimiliki Edomu kana kwamba anatupa kiatu kwa ishara katika nchi kuonesha kuwa inaimiliki. Ingawa tafsiri zingine hapa ziko tofauti. "Ninachukua umiliki wa nchi ya Edomu" au "Ninatupa kiatu changu katika nchi ya Edomu kuonesha kuwa ni yangu"

Psalms 60:10

Lakini wewe, Mungu, haujatukataa?

Mwandishi anatumia swali hili kueleza huzuni yake kuwa inaonekana kwamba Mungu amewakataa. "Lakini Mungu, inaonekana kama umetukataa." au "Mungu, inaonekana kama umetuacha"

Hauendi vitani na jeshi letu

Mwandishi anazungumzia Mungu kusaidia jeshi lao kana kwamba Mungu huwa anapigina pamoja nao. "huwa husaidii jeshi letu tunapoenda vitani"

haufai

"hauna maana"

tutashinda

"kuwa na ushindi"

atawakanyaga chini adui zetu

Mwandishi anazungumzia Mungu kusaidia jeshi lao kuwashinda adui zao kana kwamba Mungu alikuwa akiwakanyaga adui zao. "atatusaidia kuwakanyaga chini adui zetu" au "atatuwezesha kuwashinda adui zetu"

Psalms 61

Psalms 61:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Taarifa ya Jumla:

Huu ni wimbo kuhusu uaminifu wa Mungu.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

kwenye vyombo vya nyuzi

"watu wanapaswa kucheza vyombo vya nyuzi na wimbo huu"

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Sikia kulia kwangu; jali ombi langu

Vishazi hivi viwili vinamaana sawa. "Mungu, nisikilize na ujibu ombi langu"

umezidiwa

"umeshindwa"

niongoze kwenye jiwe lililo juu zaidi yangu

Hapa mwandishi anamzungumzia Mungu kana kwamba ni mwamba mkubwa anaoweza kupanda kwa ajili ya ulinzi.

mnara imara kutoka kwa adui

Maneno yanayodokezwa "unaonilinda" yanaweza kuongezwa. "umekuwa kama mwamba imara unaonilinda dhidi ya adui wangu"

mnara imara

Hapa mwandishi anamzungumzia Mungu kana kwamba ni "mnara imara" unaotoa ulinzi dhidi ya adui zake.

Psalms 61:4

nitakimbilia chini ya kivuli cha mbawa zako

Kwenda kwa Yahwe kwa ajili ya ulinzi inazungumziwa kama kumkimbilia. Hata kuna sitiari ya pili inayozungumzia ulinzi wa Yahwe kana kwamba ni kuku analinda vifaranga wake chini ya mbawa zake. "kwenda kwako kwa ajili ya ulinzi kama kifaranga alivyo salama chini ya mbawa za mama yake"

umenipa urithi

Mwandishi anazungumzia baraka za Mungu kana kwamba ni urithi aliopokea. "umenipa baraka"

wanaoheshimu jina lako

Hapa "jina lako" linamaanisha Mungu mwenyewe. "wanaokuheshimu wewe" au "walio na heshima ya ajabu kwa ajili yako"

Psalms 61:6

Utarefusha ... vizazi vingi

Vishazi hivi viwili vina maana ya kufana. Wazo linarudiwa kwa ajili ya mkazo.

Utarefusha maisha ya mfalme

"Utasababisha maisha ya mfalme kudumu muda mrefu"

miaka yake itakuwa kama vizazi vingi

Hapa "miaka" inamaanisha muda ambao mfalme ataishi. "ataishi kwa vizazi vingi"

Atabaki mbele ya Mungu milele

Hapa "kubaki mbele ya Mungu" inamaana kuwa katika uwepo wa Mungu au kuwa pamoja na Mungu. "Mungu atakuwa naye milele" au "Mungu atakuwa na mfalme milele"

Psalms 61:8

Nitaimba sifa kwa jina lako milele

Hapa "jina" linamaanisha Mungu mwenyewe. "Nitaimba sifa kwako milele"

nadhiri zangu

Hii zinamaanisha ahadi ya kutoa sadaka kwa Mungu kila siku.

Psalms 62

Psalms 62:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Taarifa ya Jumla:

Zaburi hii ni wimbo kuhusu uaminifu wa Mungu.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Yeduthuni

Mmoja wa wanamuzi wakuu wa Daudi alikuwa na jina hili. Hii inaweza kumaanisha ni yeye.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

wokovu wangu unatoka kwake

"yeye ndiye anayeniokoa"

Yeye pekee ni mwamba wangu na wokovu wangu

Mwandishi anazungumzia uwezo wa mungu kumlinda kana kwamba Mungu ni mwamba. "Yeye pekee ndiye anayeweza kunilinda na kuniokoa"

yeye ni mnara wangu wa juu

Mwandishi uwezo wa Mungu kumlinda kana kwamba Mungu ni mnara wa juu. "ananiepusha na kushikwa na adui"

sitasogezwa sana

"hakuna kitu kinachoweza kunisogeza kamwe"

Psalms 62:3

nyie wote

"adui zangu" au "adui zangu wote"

Hadi lini ... utamshambulia mtu ... au ua inayotikisika?

Hakuna mtu anayetarajiwa. "Inaonekana kama adui zangu hawataacha kunishambulia. Nijishisi kuwa myonge dhidi yako kama ukuta ulioegemea au ua uliovunjika."

utamshambulia mtu

"utanishambulia"

Watashauriana naye ili

Wanakusudia" au "Wanapanga"

Watashauriana naye ... kumletachini ... wanambariki ... mlaani

Katika mistari hii, Daudi alieleza mwenyewe kama mtu mwingine.

kwa midomo yao

Hii inamaanisha hotuba ya maneno yao.

mioyoni mwao

Hii inamaanisha mawazo yao.

Psalms 62:5

kwa kuwa matumaini yangu yako kwake

"kwa kuwa ninaweka matumaini yangu kwake"

Yeye pekee ni mwamba wangu na wokovu wangu; yeye ni mnara wangu wa juu

Mwandishi anamzungumzia Mungu kana kwamba ni mwamba na mnara wa juu. Sitiari zote hizi mbili zinaonesha jinsi Mungu anavyotoa ulinzi kutoka kwa adui wa mtu. Hapa "wokovu" inamaanisha Mungu anamwokoa mwandishi.

sitasogezwa

"hakuna kitu kinachoweza kunisogeza"

Psalms 62:7

mwamba wa nguvu yangu na kimbilo langu liko katika Mungu

Mwandishi anamzungumzia Mungu kana kwamba ni mwamba unaomlinda mtu dhidi ya adui zake. Anamzungumzia Mungu pia kana kwamba ni kivuli kinachotoa ulinzi. "Mungu huwa ananipa nguvu na ulinzi"

mwaga moyo wako

Hii inamaanisha kumwambia Mungu hisia zako za ndani kana kwamba ni kumwaga kimiminiko. "mpe Mungu mawazo yako ya ndani"

kimbilio letu

Neno "letu" linamaanisha Daudi na watu anaozungumza nao.

Psalms 62:9

wa msimamo wa chini ... watu wa msimamo wa juu ni uongo

Hii inamaanisha viwango vya utajiri na umuhimu. Misemo "ni ubatili" na "ni uongo" ina maana moja. Mtu hawezi kumwamini mtu kwa ujasiri. "huwezi kuweka imani yako kwa watu, hata kama wana umuhimu gani"

kupimwa pamoja, ni nyepesi kuliko ubatili

Ukiwaweka watu wote wa aina hii pamoja katika mizani, hawatakuwa na uzito. Hii inamaanisha kuwa hawana uthamani wa kweli kwako.

udhalimu au wizi

Maneno haya mawili yana maana moja. Huwezi kutumaini katika fedha unayochukua kutoka kwa watu wengine.

kwa kuwa hawatazaa matunda

Mwandishi anazungumzia utajiri kana kwamba ni miti au mizabibu inayoweza kuzaa matunda. "kwa kuwa hawatatoa chochote kizuri kwa ajili yako"

usiweke moyo wako kwao

Hapa "kuweka moyo wako" ni lahaja inayomaanisha kutamani kitu sana. "usiwatamani"

Psalms 62:11

Mungu amezungumza mara moja, mara mbili nimesikia hivi

Hii inamaanisha kuwa Mungu amesema hivi zaidi ya mara moja.

nguvu ni ya Mungu

"Mungu ndiye myenye nguvu kweli kweli"

Pia kwako, Bwana, ni uaminifu wa agano

"yeye ndiye anayetupenda kwa uaminifu, kama alivyoahidi"

kwa kuwa unamlipa kila mtu kwa kile alichokifanya

Mwandishi anazungumzia dhawabu za Mungu kana kwamba analipa mshahara wa kazi.

Psalms 63

Psalms 63:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

kwa bidii

"kwa uaminifu"

nafsi yangu ina kiu na wewe, na mwili wangu una shuku na wewe

Vishazi hivi viwili vinamaana mojana vinatumikapamoja kusisitiza jinsi mwandishi anavyotamani kuwana Mungu. "mwili wangu wote unatamani kuwa na wewe"

nchi kavu na iliochoka

"jangwa kavu lenye joto"

Psalms 63:3

midomo yangu itakusifu

Hapa "midomo" inamwakilisha mtu mzima. "nitakusifu"

nitainua mikono yangu katika jina lako

Hapa "katika jina lako" inamaanisha "kwako." "nitakuabudu wewe na kuomba kwako"

Psalms 63:5

Itakuwa kana kwamba nimekula mlo wa uboho na mafuta

Hapa mwandishi anazungumzia kumjua na kumwabudu Mungu kama kuridhisha zaidi ya kula chakula kizuri. "Nitakuwa na furaha zaidi ya mtu anayekula mlo wa mafuta na chakula kizuri"

kwa midomo ya furaha mdomo wangu utakusifu

Hapa "kwa midomo ya furaha mdomo wangu" inamwakilisha mtu mzima atakayemsifu Mungu kwa furaha"

ninapokuwaza kitandani mwangu ... katika masaa ya usiku

Vishazi hivi viwili vina maana sawa. Mawazo yanarudiwa kusisitiza jinsi mwandishi anavyowaza kuhusu Mungu.

Psalms 63:7

nitafurahi katika kivuli cha mbawa zako

Mwandishi anamzungumzia Mungu kana kwamba ni ndege anayelinda makinda yake chini ya mbawa zake. "ninafurahi kwa sababu unanilinda"

Nang'ang'ania kwako

"Ninakuhitaji" au "Ninakutegemea"

mkon wako wa kuume unanibeba

Hapa, mkono wa kuume unatumika kama ishara ya nguvu na uwezo. "unanibeba" au "unaniinua juu"

Psalms 63:9

wataenda chini kwenye sehemu za chini zaidi za dunia

Hii inamaanisha kuwa watakufa na kwenda sehemu ya wafu. "watakufa na kushuka katika sehemu ya wafu" au "watakufa na kwenda chini katika sehemu ya wafu"

watapewa kwa wale ambao mikono yao hutumia upanga

Hapa "upanga" inawakilisha kifo vitani, na "wale ambao mikono yao hutumia upanga" inamaanisha adui ambao wanawaua vitani. "Mungu atawasababisha kufa vitani"

watakuwa chakula cha mbweha

Hapa wanaozungumziwa ni maiti za wale wanaokufa vitani. "mbweha watakula miili yao iliyokufa"

mbweha

"mbweha" ni aina ya mbwa pori mwenye miguu mirefu. Huwa wanakula mizoga, mawindo, na matunda.

Psalms 63:11

mfalme

Daudi anajizungumzia mwenyewe. "Mimi, mfalme wa Israeli"

anayeapa kwake ... atajivunia naye

Neno "kwake" inamaanisha Mungu.

lakini mdomo wa wale wanaozungumza uongo utasitishwa

Hapa "mdomo" inamwakilisha mtu mzima. "lakini Mungu atawanyamazisha waongo wote" au "lakini Mungu atawanyamazisha wale wanaodanganya"

Psalms 64

Psalms 64:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Taarifa ya Jumla:

Zaburi hii ni ombi la msaada.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

hifadhi

"okoa"

Nifiche na hila za siri ... ghasia za watenda udhalimu

Vishazi hivi viwili vina maana ya kufanana. Kishazi cha pili kinatoa taarifa zaidi kwa kuelezea "hila za siri" zina sauti gani.

na vurugu

"nifiche na ghasia"

ghasia

sauti ya kuchanganya ya kelele na msisimko.

Psalms 64:3

wamenoa ndimi zao kama panga

Mwandishi anazungumzia ndimi wa adui zake kana kwamba zilikuwa zimechongeka kama panga. Hapa "ndimi" inawakilisha maneno makali ambayo aduizake wamezungumza. "Vitu vikali wanavyosema vinaniumiza kama upanga mkali"

mishale yao, maneno machungu

Mwandishi anazungumzia maneno machungu ya adui zake kana kwamba ni mishale inayopigwa kwake. "maneno machungu yanayonichoma mishale"

Psalms 64:5

Nani atatuona?

Watenda maovu hawategemi jibu kwa ajili ya swali lao kwa sababu wanafikiri hakuna mtu atakaye waona. "hakuna atakayeona tunachokifanya"

Mawazo ya ndani na mioyo wa watu yana kina

Mwandishi anazungumzia "mawazo ya ndani" na "mioyo ya watu" kana kwamba ni vilindi vya maji ambavyo hakuna mtu anayeweza kuvichunguza hadi chini.

Mawazo ya ndani ... mioyo ya watu

Misemo yote hii miwili inamaanisha mawazo ya siri au ya ndani ya mtu.

Psalms 64:7

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaendelea kuwazungumzia "watenda maovu" wa 64:1.

Lakini Mungu atawapiga ... kwa mishale

Mwandishi anazungumzia adhabu ya Mungu kwa watenda maovu kana kwamba Mungu anapiga mishale kwao.

Watafanywa kujikwaa

Mwandishi anazungumzia Mungu kusababisha mipango ya kushindwa kana kwamba Mungu alikuwaakiwafanya kujikwaa katika njia zao. "Mungu atawafanya wajikwae" au "Mungu atasababisha mipango yao kushindwa'

kwa kuwa ndimi zao wenyewe ziko dhidi yao

Hapa "ndimi" inawakilisha maneno wanayosema. "kwa kuwa maneno wanayosema yako dhidi yao"

alichofanya

"kile ambacho Mungu amefanya"

Psalms 64:10

watamkimbilia yeye

Kwend akwa Yahwe kwa ajili ya ulinzi inazungumziwa kama kumkimbilia. "enda kwake kwa ajili ya ulinzi"

wanyofu wote wa moyo tajivunia kwake

Hapa "wanyofu moyoni" ni lahaja inayomaanisha wanyofu na wenye haki. "watu wote wanyofu watamsifu yeye"

Psalms 65

Psalms 65:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Taarifa ya Jumla:

Zaburi hii ni wimbo wa sifa.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Zaburi. Zaburi ya Daudi

"Hii ni zaburi aliyoandika Daudi"

Kwako, Mungu uliye Sayuni, sifa zetu zinakusubiri

Hii inazungumzia sifa kana kwamba ni mtu anayeweza kutenda kitu mwenyewe. "Kwako pekee, Mungu uliye Sayuni, tutatoa sifu zetu"

nadhiri zetu zitabebwa kwako

"tutafanya tulichokuahidi kufanya"

Udhalimu unatushinda

Mwandishi anazungumzia udhalimu kana kwamba ni mtu anayeweza kushinda au kukandamiza. "ni kana kwamba dhambi zetu wenyewe zinatushinda"

utawasamehe

Watakao "samehewa" inamaanisha ni "udhalimu."

Psalms 65:4

unayemchagua ... nyuani mwako

Maneno "unaye" na "mwako" yanamaanisha Yahwe.

aishi nyuani mwako

Hii haimaanisha kuwa mtu huyo anaishi kweli kwenye hekalu lakini ni kwamba yuko huko mara kwa mara kumwabudu Yahwe. "aabudu mara kwa mara katika hekalu lako"

Tutaridhika na uzuri wa nyumba yako, hekalu lako takatifu

"Uzuri wa nyumba yako, hekalu lako takatifu, utaturidhisha"

Tutaridhika

Hapa anayezungumziwa ni Daudi na watu anaozungumza nao.

nyumba yako, hekalu lako takatifu

"nyumba yako, ambalo ni hekalu lako takatifu"

Psalms 65:5

Katika haki

"Kwa sababu u mwenye haki"

wewe ambaye ni

"wewe ni"

wa mwisho wote wa dunia ... upande wa pili wa bahari

Misemo hii inamaana za kufanana. "kwa watu wote wanaoishi duniani kote na upande wa pili wa bahari"

wa mwisho wote wa dunia

Hii inamaanisha watu wote wanaoishi duniani kote.

Psalms 65:6

wewe uliyefungwa na nguvu

Mwandishi anamzungumzia Mungu kana kwamba alivaa nguvu yake kama mshipi. "kuonesha kuwa una uwezo sana"

kuunguruma kwa bahari, kuruka kwa mawimbi yake

Misemo hii miwili inamaana moja na inatumika pamoja kuleta hisia dhahiri kwa msikilizaji na msomaji. "mwendelezo wa bahari kuunguruma"

kuunguruma

sauti kubwa inayosababishwa na upepo na mawimbi

na ghasia

"na kutuliza ghasia"

ghasia

sauti kubwa

Psalms 65:8

ushahidi

kithibitisho au kitu cha kuonesha kuwa kitu kingine ni kweli

unafanya mashariki na magharibi kufurahi

Msemo "mashariki na magharibi" inamaanisha watu wanaoishi duniani kote. "unasababisha watu wanoishi kote kupiga kelele kwa furaha"

kusaidia dunia

Hii inamaanisha udongo wa dunia.

unairutubisha sana

"unaufanya udongo kuwa mzuri sana ili vitu vizuri visitawi juu yake"

mto wa Mungu umejaa maji

Hii inamaanisha maji yaliyoko angani ambayo Mungu hutuma kumwagilia dunia na kuijaza mikondo. "unaijaza mikondo na maji"

Psalms 65:10

Unamwagilia ... lako

Anayezungumziwa hapa ni Yahwe.

mitaro yake

"mitaro ya dunia"

mitaro

Mtaro ni mfereji mrefu mwembamba unatengenezwa kwenye ardhi kwa ajili ya kupanda mbegu au kwa ajili ya kumwagilia shamba ambapo nafaka zimepandwa.

migongo

makali

Unauvika taji mwaka kwa uzuri wako

Hapa "mwaka" umepewa sifa ya kibinadamu ya kuvaa taji. "Umeupa heshima mwaka kwa mavuno mazuri"

hudondosha unono chini duniani

Neno "unono" unaashiria urutubisho au uzuri. Kama inavyotumika katika mesmo huu, inaonesha jinsi Yahwe anavyoufanya udongo kuwa mzuri sana na wenye urutubisho hadi unatoa mavuno mengi.

Malisho ... dondosha umande

Kuna umande mwingi sana katika malisho hadi yanasemwa kuudondosha. "Malisho ... yamejaa umande" au "Umande mwingi unadondoka katika malisho ya nyikani"

vilima vimevikwa na furaha

Mwandishi anazungumzia uzuri wa vilima kana kwamba ni watu wenye furaha, na furaha kana kwamba ni mavazi. "vilima ni kama watu waliovaa furaha" au "vilima ni kama watu wenye furaha"

Psalms 65:13

Malisho yamevikwa kundi

Mwandishi anazungumzia malisho kama vile yamefunikwa na kundi la kondoo hadi inakuwa kama malisho yamevaa vazi.

malisho

kiwanja kikubwa ambapo wanyama hula nyasi

kundi

kundi la wanyama, kama kondoo na mbuzi

yanapiga kelele kwa furaha, na yanaimba

Malisho, vilima na mabonde ni mengi sana hadi yanaonekana kama yanapiga kelele na kuimba kwa furaha. "ni kama watu wanaoimba kwa furaha"

yanapiga kelele

Yanayopiga "kelele" ni malisho na mabonde.

Psalms 66

Psalms 66:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Taarifa ya Jumla:

Zaburi hii ni wimbo wa sifa.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Fanya sauti ya furaha kwa Mungu, dunia yote

"Sauti ya furaha kwa Mungu" inawakilisha kuimba na kupiga kelele za kumsifu Mungu. "Acha dunia yote iimbe na kupiga kelele kwa furaha kwa Mungu"

dunia yote

Hii inamaanisha watu wote wanaoishi duniani. "watu wote duniani"

Imba utukufu wa jina lake; fanya sifa yake kuwa tukufu

Misemo hii inamaana za kufanana na inatumika kwa pamoja kusisitiza jinsi Mungu alivyo wa ajabu. "Imba kuhusu jinsi jina la Mungu lilivyo la ajabu; imba sifa ya ajabu ya jinsi Mungu alivyo mkuu"

utukufu wa jina lake

JIna la Mungu hapa linamwakilisha Mungu mwenyewe. "utukufu wake"

Psalms 66:3

Matendo yako yanaogofya

Matendo ya Mungu yanatusababisha kuwa katika mshangao na kuogopa kwa sababu tunajua kuwa ana uwezo na ni mtakatifu.

Kwa ukuu wa uwezo wako

"Kwa sababu una uwezo mkuu"

Dunia yote itakuabudu

Hii inamaanisha watu wote wanaoishi duniani. "Watu wote duniani watakuabudu"

wataimba kwa jina lako

Hapa "jina lako" linamaanisha Mungu mwenyewe. "watakusifu na kukupa heshima"

Psalms 66:5

anatisha ... yake ... kwake

Hapa anayezungumziwa ni Mungu.

anatisha

"wa ajabu"

wanadamu

"binadamu"

Aligeuza bahari kuwa nchi kavu; walipita mto kwa miguu

Hii inamaanisha kuvuka bahari ya Shamu.

walipita

Waliopita ni watu wa Mungu, Waisraeli.

tulifurahi

Waliofurahi ni Waisraeli, mababu zao, Daudi, na watu anaozungumza nao.

macho yake yanatazama

Msemo huu "macho yake" inamaanisha Mungu mwenyewe. "anaona"

usiwaache wakaidi wajiinue

"usiwaache watu wakaidi wajiinue" au "usiwaache watu wakaidi wawe na kiburi"

Psalms 66:8

Mpe Mungu baraka ... acha sauti ya sifa yake isikike

Misemo hii miwili ina maana za kufanana. Wazo linarudiwa kusisitiza umuhimu wa kumsifu Mungu.

yetu

Katika mstari huu "yetu" inajumuisha Daudi na watu anaozungumza nao.

haruhusu miguu yetu kuteleza

Mwandishi anazungumzia ulinzi wa Mungu kama kuwaepusha watu wake kuteleza wanapotembea au kuanguka katika mteremko wa ghafla. "hajaturuhusu kuanguka katika maafa"

Psalms 66:10

Umetuleta kwenye wavu

Mwandishi anazungumzia adhabu ya Mungu kana kwamba Mungu aliwashika watu wake katika wavu.

wavu

mtego kwa ajili ya ndege au mnyama

umeweka mzigo mkubwa viunoni mwetu

Mwandishi anazungumzia kile ambacho watu wamestahamili kama kulazimika kubeba mizigo mizito migongoni mwao.

Umewafanya watu kuendesha juu ya vichwa vyetu

Hii ni picha ya kushindwa vibaya vitani. "Ni kana kwamba adui zetu wametushinda vitani na wameendesha vibandawazi vyetu juu ya miili yetu iliyoanguka"

tulipita katika moto na maji

Mungu aliwajaribu kwa maafa ya asili kama moto na mafuriko. "tuliteseka kama watu wanavyoteseka kutokana na moto na mafuriko"

sehemu yenye nafasi

Mwandishi anazungumzia baraka walizonazo sasa watu wa Israeli kana kwamba wameletwa katika nafasi kubwa ya wazi ambapo wako salama. "nafasi ya wazi ambapo tuko salama"

Psalms 66:13

ambazo midomo yangu iliahidi na mdomo wangu kuzungumza

Hapa "midomo" na "mdomo" inamaanisha maneno ya ahadi yaliyozungumzwa. "niliyoahidi"

harufu nzuri ya kondoo dume

"harufu ya moshi wa kondoo dume wa sadaka"

Psalms 66:16

Nitatangaza alichofanya kwa ajili ya nafsi yangu

Neno "nafsi" linamwakilisha mtu mzima. "Nitakwambia alichofanya kwa ajili yangu"

Nililia kwake kwa mdomo wangu

Neno "mdomo" linamwakilisha mtu mzima. anayelia kwa Mungu.

alisifiwa kwa mdomo wangu

Hpa "ulimi" unawakilisha maneno au hotuba. "Nilimsifu kwa ulimi wangu" au "Nilimsifu"

ningeona dhambi

"ningependa dhambi" au "kutunza udhalimu"

asinge nisikiliza

Hapa "asinge nisikiliza" inadokeza kuwa Mungu asinge jibu ombi lake. "asinge nisikia nikimwita" au "asinge jibu ombi langu"

Psalms 66:19

Lakini hakika Mungu amesikia; amevuta nadhari

Vishazi hivi viwili vina maana za kufanana na zinatumika pamoja kusisitiza kuwa Mungu amesikia ombi lake. "Lakini hakika Mungu amesikia ombi langu"

sauti ya ombi langu

Hapa ombi la mwandishi limepewa sifa ya kuwa na sauti. "ombi langu"

au uaminifu wake wa agano kutoka kwangu

"au kugeuza uaminifu wake wa agano kutoka kwangu"

Psalms 67

Psalms 67:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

kwenye vyombo vya nyuzi

"watu wanapaswa kucheza vyombo vya nyuzi na wimbo huu"

kusababisha uso wake ung'ae kwetu

Mwandishi anamzungumzia Yahwe kuwatendea fadhila kana kwamba uso wa Yahwe uling'aa mwanga juu yao. "kututendea fadhili"

njia zako zijulikane duniani

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "watu wajue njia zako duniani"

wokovu wako miongoni mwa mataifa yote

Mwandishi anatamani kila mtu ajue kuwa Mungu ana uwezo wa kuwaokoa. Hii inaweza kuwekwa wazi. "na watu wa mataifa yote wajue kuwa una uwezo wa kuwaokoa"

Psalms 67:3

Achawatu wakusifu ... acha watu wakusifu

Kishazi cha pili kinaogenza uzito wa maana ya ile ya kwanza kwa kusisitiza umuhimu wa kumsifu Mungu.

acha mataifa ... tawala mataifa

Hapa "mataifa" yanamaanisha watu wanaoishi katika mataifa yote duniani.

kwa haki

"kwa usawa"

Psalms 67:5

Achawatu wakusifu ... acha watu wakusifu

Kishazi cha pili kinaogenza uzito wa maana ya ile ya kwanza kwa kusisitiza umuhimu wa kumsifu Mungu.

Nchi imetoa mazao yake

Hapa mwandishi anazungumzia "dunia" kana kwamba imechagua kutoa mazao kwa watu. "Tumevuna mazao mengi kutoka kwenye mazao yetu.

Psalms 67:7

na mwisho wote wa dunia unamheshimu

Hii inamaanisha kwamba watu kila sehemu wanapaswa kumheshimu Mungu kwa sababu ya baraka zake. "ninatamani kwamba watu wote kila mahali duniani wawe na heshima ya ajabu kwake"

Psalms 68

Psalms 68:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Acha Mungu ainuke

Mungu kuanza kutenda inazungumziwa kana kwamba anasimama. "Acha Mungu aanze kutenda"

acha adui zake watawanyike

"acha Mungu awafukuze adui zake"

Kama moshi unavyopeperushwa, ndivyo hivyo uwapeperushe

Adui wa Mungu wanazungumziwa kana kwamba ni moshi unaoweza kupeperushwa kwa urahisi na upepo. "Waondoe kama upepo unavyopuliza moshi"

kama nta inavyoyeyuka mbele ya moto

Adui wa Mungu wanazungumziwa kana kwamba ni nta inayoyeyuka kwa wepesi na moto. "wasababishe kupotea kama nta inavyoyeyuka mbele ya moto.

waovu

Hii inamaanisha watu waovu kwa ujumla.

wenye haki

Hii inamaanisha watu wenye haki kwa ujumla.

wafurahi na kushangilia

Hii inamaanisha kitu kimoja na inasisitiza kiasi cha furaha walichokuwanacho.

Psalms 68:4

jina lake

Hii inamaanisha Mungu. "kwake"

yule anayeendesha katika sehemu za wazi

Uwepo wa Mungu katikati ya watu unazungumziwa kana kwamba anaendesha juu ya dunia katika farasi au kibandawazi.

Baba wa wasio na baba

Mungu anazungumziwa kama Mungu mwenye huruma anayekuwa kama baba kwa yatima. "Yule anayekuwa kama baba kwa watoto wasio na wazazi"

mwamuzi wa wajane

Mungu anazungumziwa kama Mungu anayewlinda wajane. "mlinzi wa wajane"

Mungu huwaweka wapweke katika familia

Mungu anazungumziwa kana kwamba huwaweka watu wapweke katika familia. "Mungu huwapa familia wale waiokuwa na mtu wa kuishi nao"

huwaleta nje wafungwa kwa kuimba

Mungu anazungumziwa kama yule anayewaongoza wafungwa kutoka katika vifungo vyao. "Mungu huwaweka huru wafungwa na huwafanya waimbe kwa furaha"

wakaidi

Hii inamaanisha watu wakaidi. "wale wanaokaidi dhidi yake"

nchi kavu

Adhabu ya Mungu kwa wakaidi inazungumziwa kana kwamba anawalazimisha kuishi katika jangwa lenye joto. "nchi kavu na yenye joto kali"

Psalms 68:7

Taarifa ya Jumla:

Daudi anaanza kueleza hadithi ya Mungu kuwaongoza Waisraeli katika jangwa hadi mlima Sinai.

ulipotoka nje ... ulipotembea katika

Misemo hii miwili inamaanisha tukio lile lile.

ulipotoka nje mbele ya watu wako

"uliwaongoza watu wako"

ulipotembea katika nyika

Mungu anazungumziwa kana kwamba ni askari anayetembea mbele ya watu wa Israeli.

mbingu pia zikadondosha mvua ... uwepo wa Mungu

"Mungu alisababisha inyeshe"

katika uwepo wa Mungu

Lahaja hii inamaanisha kutokea kwa Mungu mbele ya Waisraeli. "Mungu alipotokea kwa Waisraeli"

Psalms 68:9

uliimarisha urithi wako ulipochoka

Nchi ya Israeli inazungumziwa kana kwamba ni mtu anayeweza kuchoka, au kuptat nguvu. "ulisababisha nchi kutoa mazao mazuri"

urithi wako

Nchi ambayo Mungu aliwapa Waisraeli inazungumziwa kana kwamba ni urithi ambao baba alipitisha kwa watoto wake. "nchi uliyotupa sisi Waisraeli"

maskini

Hii inamaanisha watu maskini kwa ujumla. "watu maskini"

Psalms 68:11

Taarifa ya Jumla:

Daudi anaendelea hadithi ya safari ya Waisraeli katika jangwa. Katika sehemu hii ya hadithi, Waisraeli wanashinda vitani dhidi ya adui zao.

wale walioyatangaza ... jeshi kubwa

Idadi kubwa ya watu walisema ujumbe wa Bwana kwa wengine. Wanazungumziwa kana kwamba ni jeshi kubwa. Kwa kuwa msemo huu ni wa kike, tafsiri zingine hutafsiri hii kama, "wanawake walioyatangaza ... jeshi kubwa."

Wafalme wa majeshi ... kwa nini mlifanya hivi?

Taarifa hii katika 68:11 imepangwa vingine ili maana yake ieleweke kwa wepesi zaidi.

Wafalme wa majeshi wanatoroka, wanatoroka

Wafalme wanawakilisha majeshi kamili. Inaeleweka kuwa wanatoroka kwa sababu wameshindwa na jeshi la Israeli. "Wafalme na majeshi yao wanatutoroka kwa sababu wameshindwa"

nyara

mali vinavyochukuliwa kutoka kwa jeshi lililoshinwa na kuletwa kwa maskani ya jeshi lililo shinda.

njiwa waliofunikwa kwa fedha ... dhahabu

Hii inamaanisha kuwa baadhi ya vitu vilivyotekwa nyara ni vya thamani sana kwa sabau vimefunikwa kwa mawe ya thamani.

Wakati baadhi ya nyie watu mlipobaki katika zizizi za kondoo, kwa nini mlifanya hivi?

Swali hili linatumika kukemea watu ambao hawakushiriki vitani. "Wale waliobaki katika zizi za kondoo wasinge baki; wangeenda vitana."

Psalms 68:14

aliwatawanya wafalme huko ... anguka theluji juu wa mlima Salmoni

Kuna wafalme na askari wengi sana waliokufa katika mlima hadi wanazungumziwa kana kwamba ni theluji iliyofunika mlima. "aliwashinda wafalme na askari wengi sana huko hadi wakawa kama chembe za theluji imefunika mlima Salmoni."

aliwatawanya wafalme

Hapa "wafalme" inamaanisha majeshi pia. "aliwatawanya wafalme adui na majeshi yao"

mlima Salmoni

HIli ni jina la mlima.

Mlima mkuu ni ... mlima wa juu ni

Misemo hii miwili inamaana za kufanana na inatumika pamoja kuimarisha nyingine. "mlima mkuu na wa juu ni nchi ya kilima cha Bashani"

Kwa nini unaangalia kwa wivu ... kwa ajili ya sehemu atakayoishi?

Swali hili linawezakuandikwa kama kauli. "Nchi ya kilima cha juu cha Bashani hakitakiwa kuangalia kwa wivu mlima wa ambao Mungu anatamani kwa ajili ya sehemu atakayoishi."

Psalms 68:17

elfu ishiri, maelfu juu ya maelfu

Hii inawezekana haimaanishi idadi kamili, lakini kuashiria idadi kubwa. "maelfu mengi"

unapanda

Hii ni kwenda juu kuelekea angani.

Psalms 68:19

hubeba mizigo yetu kila siku

"hubeba mizigo yetu mizito kila siku." Kujali kwa Bwana kwa ajili ya watu wake inazungumziwa kana kwamba alikuwa akibeba kwa uhalisia matatizo yao kama mzigo.

Mungu ambaye ni wokovu wetu ... Mungu wetu ni Mungu anayeokoa

Misemo inamaanisha kitu kimoja. "Mungu anayetuokoa ... Mungu wetu ni Mungu anayeokoa"

atapiga katika vichwa vya adui zake

Mungu anazungumziwa kana kwamba ni shujaa ambaye ataua adui zake kwa kuwapiga vichwani ili kuwaua. "atawaua adui zake kwa kuwapiga kichwani"

ngozi ya kichwa na nywele nyingi

Inaonekana kuwa utamaduni wa wanajeshi kutonyoa nywele zao wakati wa vita. "mafuvu yenye nywele ndefu"

wanaotembea katika makosa dhidi yake

Kumkosea Mungu inazungumziwa kama kutembea kwenye makosa. "kumkosea mara kwa mara"

Psalms 68:22

nitawarudisha

Watakaorudishwa ni adui wa Mungu.

vilindi vya bahari

Hii ni lahaja inayomaanisha sehemu za mbali za duniani ambapo watu watajaribu kumtoroka Mungu.

uwaponde adui zako

Uharibifu wa adui wa Israeli unazungumziwa kana kwamba Waisraeli waliwagandamiza chini ya miguu yao. "kuwashinda kabisa adui zako"

unachovya mguu wako kwenye damu

Vurugu ya kutoka kwenye uharibifu wa adui unazungumziwa katika njia ya picha kali, kana kwamba Waisreali watakuwa wakisimama katika damu ya adui zao waliokufa. "kukanyaga katika damu yao"

ndimi za mbwa wako wawe na gao lao

Umwagaji wa damu katika vita dhidi ya adui wa Israeli unazungumziwa kana kwamba ni mkubwa sana hadi mbwa watalamba damu inayotiririka kwa ndimi zao.

Psalms 68:24

maandamano

Maandamano ni kundi kubwa la watu wanaotembea pamoja kwa mpangilio kama sehemu ya sherehe.

wapiga vinanda

watu wanopiga vyombo vya muziki

Psalms 68:26

Mbarikini Mungu katika mkusanyiko; msifuni Yahwe, nyie uzao wa kweli wa Israeli

"Nyie ambao ni kizazi cha kweli cha Israeli, msifuni Yahwe na mbarikini Mungu katika kusanyiko.

makundi yao

"kundi lao." Neno "lao" linamaanisha viongozi wa Yuda.

Psalms 68:28

Mungu wenu, Israeli, ameagiza nguvu yenu

Tafsiri zingine zinaelewa maandiko ya Kihebrania tofauti. "Amrisha (au tumia) nguvu yako, Mungu"

Mungu wenu, Israeli, ameagiza

"Watu wa Israeli, Mungu wenu ameagiza"

kwetu

Neno "kwetu" linamaanisha watu ambao Daudi anazungumza nao na yeye mwenyewe.

Onesha uwezo wako kwetu kutoka katika hekalu lako Yerusalemu

Unapokuwepo katika hekalu lako Yerusalemu, tuoneshe uwezo wako"

Onesha uwezo wako

"Tuonesha kuwa una nguvu"

Psalms 68:30

wanyama pori katika matete

Wasomi wengi wanaamini wanyama pori hawa ni sitiari inayomaanisha watu wa Misri. "watu wa Misri ambao ni kama wanyama pori katika matete"

watu, makundi ya mafahali na ndama

Watu wa mataifa mengine wanazungumziwa kana kwamba ni kundi kubwa la ngombe. "mataifa yenye nguvu, ambao ni kama makundi ya mafahali"

watawanye

kusambaza au kusababisha kitu kusambaa haraka katika pande tofauti

Wakuu watatoka kutoka Misri

Inadokezwa kuwa wakuu wanatoka Misri ili kumpa Mungu zawadi Yerusalemu. "Kisha viongozi wa Misri wataleta zawadi kwako"

Kushi

Hii inamaanisha watu wa Kushi. "Watu wa Kushi"

anafika kwa mikono yake kwa Mungu

Hili tendo linaloashiria kumwabudu Mungu. "anainua mikono yake kumsifu Mungu"

Psalms 68:32

nyie falme za duniani

Hapa "falme" inamaanishwa wakazi wa falme. "nyie watu ambao ni wakazi wa falme duniani kote"

Kwake anayeendesha juu ya mbingu ya mbingu

Neno "Imbeni" linadokezwa kama mwanzo wa mstari huu. Hapa Mungu anaelezwa kana kwamba anaendesha kibandawazi angani. "Imbeni kwa Mungu anayeendesha juu ya anga katika kibandawazi chake"

anainua sauti yake kwa nguvu

Lahaja hii inamanisha anazungumza kwa nguvu. "anapiga kelele kwa nguvu" au "anazungumza kwa sauti kubwa"

Psalms 68:34

Mhesabieni Mungu nguvu

"Mhesabieni" inamaanisha kumpa mtu sifa. "Nguvu ni ya Mungu"

nguvu yake iko angani

"katika anga pia anaonesha kuwa ana uwezo"

Mungu, wewe unatisha katika sehemu yako takatifu

Hapa mwandishi anazungumza moja ka moja na Mungu.

nguvu na uwezo

Maneno haya mawili yana maana moja. Yanasisitiza kiasi ambacho Mungu anawapa nguvu watu wake.

Psalms 69

Psalms 69:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Taarifa ya Jumla:

Zaburi hii ni ombi la msaada.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

weka katika Shoshannimu

Hii inaweza kumaanisha mtindo wa muziki.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

kwa kuwa maji yameweka maisha yangu hatarini

Mwandishi anaelezea matatizo maishani mwake kana kwamba alikuwa akizama kwenye mafuriko ya maji. "kwa kuwa ni kama ninazama katika maji"

ninazama katika matope mengi

Mwandishi anaelezea matatizo maishani mwake kana kwamba anazama katika matopemengi. "Kwa kuwa ni kama ninazama katika matope mengi na nitakufa"

matope

udongo wa maji maji

hakuna sehemu ya kusimama

Mwandishi anatumia kauli hasi kusisitiza jinsi hali ilivyokuwa haiko imara na haileweki.

Nimekuja katika maji marefu, ambapo mafuriko yanapita juu yangu

Mwandishi anaelezea matatizo yake kana kwamba anazama katika mto mrefu wenye vurugu. "nahisa kama niko kwenye maji marefu, na mafuriko ya maji yanapita juu yangu"

Psalms 69:3

nimechoka

kuchoka sana

macho yangu yameshindwa

Lahaja hii inamaanisha kuwa mwandishi amaelia sana hadi macho yake hayaoni vizuri tena. "macho yangu yamevimba kutokana na machozi"

zaidi ya nywele kichwani mwangu

Hii ni kukuza kwa neno kuonesha ni kisasi gani cha adui alichonacho mwandishi. "zaidi ya niwezavyo kuhesabu, kama nywele kichwani mwangu"

nikata

Lahaja hii inamaanisha "niue."

Psalms 69:5

upumbavu wangu

"vitu vya kipumbavu ambavyo nimefanya"

dhambi zangu hazijafichwa kutoka kwako

"unajua dhambi zangu zote"

wale wanaokusubiri wewe waaibishwe ... wale wanakutafuta wakose heshima

Misemo hii miwli inamaana moja na inasisitiza hamu ya mwandishi ya kwamba Mungu awalinde watu wake.

Usiache wale wanaokusubiri wewe waaibishwe kwa sababu yangu

"Tafadhali usiwaaibishe wale wanaokusubiri wewe kwa sababu yangu"

Usiache wale

"Usiwaache wale"

usiache wale wanakutafuta wakose heshima kwa sabau yangu

"Tafadhali usiwenyime heshima kwa sababu yangu wale wanaokutafuta wewe"

wale wanakutafuta

Kumtafuta Mungu inawakilisha kati aya 1) kumwomba Mungu msaada au 2) kuwaza kumhusu Mungu na kumtii. "wale wanao omba msaada wako" au 2) wale wanaokuabudu na kukutii wewe"

Psalms 69:7

Kwa ajili yako

"Kwa niaba yako"

Nimebeba lawama

Lawama za adui wa mwandishi zinazungumziwa kana kwamba ni mzigo mzito ambapo alitakiwa kubeba. "Nimevumilia matusi ya adui zangu"

aibu imefunika uso wangu

Mwandishi anazungumzia aibu anayoihisi kana kwamba ni kitu kibaya usoni pake ambacho kila mtu anakiona vizuri. "Nimeaibika sana"

Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu

Mwandishi anajizungumzia mwenyewe kana kwamba hakuwa sehemu ya familia yake mwenyewe. "Ndugu zangu hawanijui tena au kunikubali kabisa"

mgeni kwa ndugu zangu ... mgeni kwa watoto wa mama yangu

Misemo hii miwili inamaana moja. Inarudiwa kusisitiza mtengano na familia yake mwenyewe.

mgeni kwa watoto wa mama yangu

Mwandishi anajizungumzia mwenyewe kana kwamba hakuwa sehemu ya familia yake mwenyewe. "ndugu zangu hawanijui tena au kuniamini kabisa"

ari ya nyumba yako imenila

Mwandishi anazungumzia ari kwa ajili ya hekalu la Mungu kana kwamba ni mnyama pori unaommeza mwandishi. "ari niliyonayo kwa ajili ya nyumba yako inanimeza"

imenila

Lahaja hii inamaanisha ari ya mwandishi kwa ajili ya hekalu inateka mawazo na matendo yake yote. "inatawala kabisa kila kitu nachowaza na kufanya"

lawama ... zimeniangukia

Mwandishi anazungumzia lawama za adui wa Mungu kana kwamaba ni mawe yaliyopondwa kwa mwandishi. "wale wanaokulaumu piwa wanatuma lawama zao kwangu"

Psalms 69:10

Nililia na sikula chakula

Ukweli kuwa mwandishi alikuwa akifunga inaashiria kuwa alikuwa na huzuni kuhusu jinsi watu walivyolitendea hekalu la Mungu.

walinidhihaki

"adui zangu walinilaumu kwa sababu yake"

nilipofanya magunia kuwa mavazi yangu

Kuvaa vnguo mbaya, za thamani ndogo ni ishara ya kuomboleza juu ya dhambi.

nikawa kitu cha mithali

Mwandishi anajizungumzia kana kwamba alikuwa ndiye mtu mwenye huzuni au mpumbavu katika mithali. "nikawa mfano wa mtu mwenye huzuni anayezungumziwa katika mithali" au "wananicheka"

Wale wanokaa katika lango la mji

Hapa "lango la mji" unahusishwa na uongozi wa mji. "Watu muhimu wa mji"

mimi ni wimbo wa walevi

Mwandishi anajizungumzia kana kwamba alikuwa ndiye mtu ambaye walevi walimkejeli kwa myimbo. "walevi wa mji wanaimba nyimbo za kuudhikunihusu mimi"

Psalms 69:13

katika muda utakaokubali

"katika muda wako uliokubalika" au "utakapokuwa tayari"

nijibu katika uaminifu wa wokovu wako

"niokoe kwa sababu unanipenda kwa uaminifu, kama ulivyoahidi kufanya"

Nivute nje ... usiniache nizame

Misemo hii miwili ina maana moja.

Nivute nje ya matope, na usiniache nizame

Mwandishi anazungumzia hatari yake kutoka kwa adui zake kana kwamba alikuwa akizama katika shimo la matope. "Usiniruhusu niendelee kuzama katika matope"

acha nichukuliwe

Hapa "kuchukuliwa" inamaanisha kutolewa kutoka hatarini. "nitoe" au "niokoe"

niokolewe kutoka

"tafadhali niokoe kutoka"

maji marefu ... mafuriko ya maji ... kilindi

Misemo hii ina maana moja.

niokoa kutoka kwenye maji marefu

Mwandishi anazungumzia hatari yake kutoka kwa adui zake kana kwamba anazama katika maji marefu.

mafuriko ya maji yamenilemea

Mwandishi anazungumzia hatari yake kutoka kwa adui zake kana kwamba mafuriko ya maji yalikuwa yakimfunika kabisa.

kilindi kinanimeza

Mwandishi anazungumzia kilindi kana kwamba ni mnyama hatari aliyekuwa tayari kumla. "maji marefu yananimeza kama mnyama hatari"

Usiruhusu shimo lifunge mdomo wake kwangu

Hapa "shimo" linazungumziwa kana kwamba lina mdomo kama mtu na linaweza kumla mwandishi. "Usiruhusu shimo linimeze" au "Usiache shimo la mauti lifunge juu yangu"

Psalms 69:16

uaminifu wako wa agano ni mzuri

"wewe ni mwema na unanipenda kwa uaminifu"

huruma zako kwangu ni nyingi

"una huruma sana kwangu"

geukia kwangu

Wazo la kumgeukia mtu linamaanisha kumvutia nadhari kwao au kuwasaidia. "nisaidie"

Usifiche uso wako kwa mtumishi wako

Kuficha uso wa mtu inamaanisha kukataa kumsikiliza au kumsaidia mtu. "Tafadhali msaidie mtumishi wako" au "Tafadhali nisaidie"

katika dhiki

"katika taabu kubwa"

Psalms 69:18

niokoe

Mwandishi anamwomba Mungu kumwokoa kana kwamba mwandishi alikuwa ni mtumwa ambaye uhuru wake ungewezz kununuliwa na Mungu.

nikomboe mateka

Mwandishi anazungumzia kulipia fidia maisha yake kana kwamba alikuwa mtumwa ambaye uhuru wake ungeweza kununuliwa kwa fedha.

lawama yangu, aibu yangu, na fedheha yangu

"jinsi watu walivyonilaumu, niaibisha, na kunifedhehesha"

adui zangu wote wako mbele zako

Hapa "mbele zako" inamaanisha kuwa Mungu anaona na kujua yote kuwahusu. "unajua adui zangu wote ni kinanani"

Psalms 69:20

imevunja moyo wangu

Lahaja hii inamaanisha mtu ana huzuni sana. "imenikosea sana"

nimeja uzito

huzuni kuu ya mwandishi inazungumziwa kana kwamba alikuwa amejaa uzito. "nimejaa uzito wa huzuni"

kunihurumia

kusikia maombolezo au huzuni

Walinipa sumu kama chakula changu

Hii inaweza kuwa fumbo. Chakula ambacho watu walimpa mwandishi kilikuwa kibaya sana hadi kilikuwa na ladha kama ya sumu. "Walinipa chakula chenye ladha kama ya sumu"

Psalms 69:22

Acha meza yao mbele yao iwemtego ... acha iwe tanzi

Mwandishi angependa kuona chakula cha adui zake kinawaharibu kabisa kana kwamba ni wanyama wadogo walionaswa katika mtego au tanzi. "Na chakula chao kiwaharibu kama mtego ... na kiwaangamize kama tanzi"

meza yao

Hii inamaanisha chakula kilichowekwa mezani, inawezekana katika karamu. "chakula chao wenyewe" au "karamu za sadaka"

Acha macho yao yatiwe giza

Mwandishi anazungumzia macho yasiyoweza kuona vizuri kana kwamba yametiwa giza. "Tafadhali uwafanye wasiweze kuona kitu"

ufanye viuno vyao vitetemeke

Migongo midhaifu inazungumziwa kana kwamba inatetemeka katika udhaifu. "sababisha migongo yao kuwa minyonge kwao kufanya lolote"

viuno vyao

"pembeni kwao" au "migongo yao"

Psalms 69:24

Mwaga gadhabu yako juu yao

Mungu kuonesha hasira yake inaelezwa kana kwamba aliimwaga juu ya adui zake kama maji.

gadhabu

"hasira kali" au "hasira'

ukali wa hasira yako

"hasira yako ya moto" au "hasira yako kali"

uwapite

Hukumu ya Mungu kwa adui zake unaelezwa kana kwamba aliwafukuza na kuwashika.

iwe ya kuhuzunisha

"kuwa imetelekezwa"

Psalms 69:26

walimtesa yule

"walimtesa mtu"

uliyempiga chini

Hapa "kupiga chini" inamaanisha adhabu. "ulimwadhibu"

wale uliowaumiza

Hapa "kuumizwa" inamaansiha kuwasababisha kuteseka. "wale uliowasababisha wateseka"

Washtakaki kwa kufanya udhalimu baada ya udhalimu

"Endelea kuweka kumbukumbu ya dhambi zao zote"

udhalimu baada ya udhalimu

"dhambi nyingi sana"

usiwaache waje katika ushindi wako wa haki

Kuja katika ushindi wa Mungu ni lahaja inayomaanisha kupokea dhawabu kutoka kwake. "usiwaache wapokee dhawabu yako ya haki"

Psalms 69:28

Acha wawekewe doa katika

Kinachozungumziwa hapa ni majina ya adui. "Futa majina yao katika"

wasiandikwe chini

"usiandike majina yao"

acha wokovu wako, Mungu, uwaweke juu

"Mungu, niokoe na uniweke katika sehemu salama"

Psalms 69:30

jina la Mungu

Hapa "jina" linamaanisha Mungu mwenyewe. "Mungu"

kwa shukrani

"kwa kumshukuru"

zaidi ya ng'ombe au fahali

"bora zaidi ya kutoa sadaka ya ng'ombe au fahali"

fahali mwenye pembe na kwato

Msemo huu unatofautisha fahali wazima na ndama wadogo. "fahali mzima mweye pembe na kwato"

Psalms 69:32

Wapole

Hii inamaanisha watu wapole kwa ujumla. "Watu wapole"

nyie mnaomtafuta Mungu

Kumtafuta Mungu inawakilisha kati ya 1) kumwomba Mungu msaada au 2) kumuwaza Mungu na kumtii. "nyie mnaomwomba Mungu msaada" au "nyie mnaomuwaza Mungu"

acha mioyo yenu iishi

Hapa "mioyo" inamaanisha watu. Hapa "kuishi" ni lahaja inayomaanisha kutiwa moyo. "na utiwe moyo"

Yahwe huwasikia

Hapa "huwasikia" inamaanisha hujibu. "Yahwe hujibu"

wahitaji

Hii inamaanisha watu wahitaji kwa ujumla. "watu wahitaji"

wafungwa wake

"wale walioteseka kwa ajili yake"

Psalms 69:34

Acha mbingu na nchi zimsifu ... bahari

Hapa mbingu na nchi na bahari zinazungumziwa kana kwamba ni watu wanaoweza kumsifu Mungu.

bahari na kila kitu kinachoenda ndani yake

"acha bahari na kila kitu kinachoenda ndani yake kimsifu Mungu"

Mungu ataiokoa Sayuni

Hapa "Sayuni" inamaanisha watu wa Sayuni. "Mungu atawaokoa watu wa Sayuni"

kuwa nayo kama mali ya kumiliki

Hapa neno "nayo" linamaanisha nchi ya Yuda.

wanaopenda jina lake

Hapa "jina" linamaanisha Mungu mwenyewe. "wanaompenda Mungu"

Psalms 70

Psalms 70:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

kuleta katika kumbukumbu

"zaburi hii iliandikwa kuwasababisha watu kukumbuka"

wale ambao

"watu ambao"

kuchukua maisha yangu

Lahaja hii inamaanisha "kuniua"

waaibike na kudhalilishwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Mungu awaweke katika aibu na kuleta fedheha juu yao"

acha wageuzwe nyuma na kuletwa kwenye fedheha

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Mungu awageuze na kuwafanya waaibike kwa yale waliyotenda"

acha wageuzwe nyuma

Kusimamishwa inazungumziwa kama kugeuzwa kutoka kwenye mashambulizi yao. "kusimamishwa"

wale wanaosema, "Aha, aha"

Hii inaonesha kudhihaki kicheko. "wale wanao nidhihaki na kunicheka"

Psalms 70:4

wanaokutafuta

Kumtafuta Mungu inaashiria kati ya 1)kumwomba Mungumsaada au 2) kumwaza Mungu na kumtii. "kukuomba msaada" au"kukuwaza na kukutii"

washereheke na kufurahi

Misemo hii miwili inamaana sawa na inasisitiza uzito wa furaha. "kufurahi sana" au "kuwa na furaha sana"

wanaopenda waokovu wako

Nomino dhahania ya "wokovu" inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "wanaokupenda kwa sababu umewaokoa"

daima waseme

Hapa ni kukuza kwa neno ili kusisitiza umihimu wa kumsifu Mungu mara kwa mara.

Mungu asifiwe

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Acha kila mtu amsifu Mungu"

maskini na mhitaji

Hapa maneno "maskini" na "mhitaji" yanamaana ya kufanana na yanasisitiza kuwahakuweza kujihudumia mwenyewe. "mhitaji sana"

harakisha kwangu

Mwandishi anamzungumzia Mungu kana kwamba anamkimbilia mwandishi ili amsaidie. "njoo upesi unisaidie!"

wewe ni msaada wangu na unaniokoa

Hapa msemo "unaniokoa" unaeleza jinsi Mungu alivyo msaada wake. "unanisaidia kwa kuniokoa"

usichelewe

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "tafadhali njoo upesi"

Psalms 71

Psalms 71:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Taarifa ya Jumla:

Zaburi hii ni ombi kwa ajili ya msaada.

Katika wewe, Yahwe, ninakimbilia

Kwenda kwa Yahwe kwa ajili ya ulinzi inazungumziwa kama kumkimbilia. "kwenda kwako, Yahwe, kwa ajili ya ulinzi"

acha nisiaibishwe kamwe

"usiwaruhusu kamwe adui zangu kuniaibisha"

unifanya kuwa salama katika haki yako

Maana zinazowezekana ni 1) "nifanye kuwa salama kwa sababu daima huwa unafanya kilocho sawa" au 2) "nifanye kuwa salama ninapofanya kile unachotaka nifanye"

geuza sikio lako kwangu

Hapa "sikio lako" inamaanisha utayari wa Mungu kumsikiliza mtu anaye omba kwake. "kuwa msikivu kwangu"

Uwe kwangu mwamba wa kukimbilia

Mwandishi anaomba kwamba Yahwe amfanye kuwa salama kama ambavyo angekuwa kama angejificha kwenye mwamba mkubwa au jabali ambapo adui zake wasingempata.

mwamba ... mwamba

Hivi ni vilima au milima, sio mawe ambayo mtu anaweza kushika mkononi.

umetoa amri

"umewaamuru malaika wako"

kuniokoa

"niweke salama"

wewe ni mwamba wangu na ngome yangu

Mwandishi wa zaburi anaamini kuwa Yahwe atamlinda na kumfanye kuwa salama kana kwamba anajificha juu ya mlima mkubwa au kwenye ngome iliyotengenezwa na mwanadamu.

Psalms 71:4

kutoka kwenye mkono wa mwovu, kutoka kwenye mkono wa asiye na haki

Maana zinazowezekana ni 1) neno "mkono" ni njia nyingine ya kusema nguvu. "kutoka katika nguvu ya wasio na haki" au 2) "mkono" unamaanisha mtu mwenyewe. "kutoka kwa watu waovu, kutoka kwa watu wasio na haki" au "ili kwamba watu waovu na watu wasio na haki hawawezi kunidhuru"

mwovu, kutoka kwenye mkono wa asiye na haki

"mwovu; niokoe kutoka kwenye mkono wa asiye na haki."

mwovu ... asiye na haki ... mkatali

"watu waovu... watu wasio na haki ... watu wakatili"

wewe ni matumaini yangu

Hapa "matumaini" ni njia nyingine ya kusema yule ambaye mwandishi wa zaburi anamtumaini. "wewe ndiye ninayekutegemea unisaidie"

Psalms 71:6

Kupitia wewe nimebebwa tangu tumboni

"Umenibeba tangu tumboni" au "Umenitunza tangu nitoke tumboni mwa mama yangu"

wewe ndiye

"wewe ndiye yule"

Mimi ni mfano kwa watu wengi

"Watu wengi wanaona ninavyoishi na wanataka kuishi kama mimi"

Psalms 71:8

Mdomo wangu umejaa na sifa yako ... na heshima yako

Mwandishi wa zaburi anazungumzia hamu yake ya kumsifu na kumpa heshima Yahwe kwa maneno anayoyazungumza kana kwamba mdomo wake umejaa maneno kama unavyoweza kujaa chakula. "Mdomo wangu utajaa maneno yanayokusifu wewe ... yanayo kuheshimu wewe" au "Nitakusifu daima ... nitakupa heshima daima"

sifa yako

"maneno yanayo waambia watu jinsi ulivyo mkuu"

heshima yako

"maneno yanayo wasababisha watu wakupe heshima"

siku nzima

"wakati wote"

Usinitupe ... usiniache

Misemo hii miwili ina maana moja na inatumika kwa pamoja kwa ajili ya mkazo.

Usinitupe

"Usinilazimisheniende mbali na wewe." Kwa Mungu kumkataa inazungumziwa kana kwamba Mungu anamlazimisha kwenda mbali. "usinikatae"

usiniache

"usiniache milele"

Psalms 71:10

angalia maisha yangu

"wanasubiri nafasi ya kuniua"

Wanasema

"Wanasema kunihusu"

mfuatilieni na kumchukua

"mfuateni anapokimbia na muueni"

Psalms 71:12

usiwe mbali nami

"kaa karibu nami"

harakisha kunisaidia

"nisaidie mapema"

Acha waaibike na kuangamia, wale walio na uhasama na maisha yangu

"Acha wale walio na uhasama na maisha yangu waaibike na kuangamizwa"

Acha waaibike na kuangamia

"Waaibishe na kuwaangamiza"

wale walio na uhasama na maisha yangu

"wale wanaonishtaki kwa kufanya kosa"

acha wafunikwe na lawama na fedheha, wale wanaotafuta kuniumiza

"acha wale wanaotafuta kuniumiza wafunikwe na lawama na fedheha"

acha wafunikwe kwa lawama na fedheha

"wafunike kwa lawama na fedheha." "na kila mtu awalaumu, na mtu yeyote asiwape heshima"

wale wanaotafuta kuniumiza

"wale wanaotafuta njia za kunidhuru"

Psalms 71:14

zaidi na zaidi

"zaidi wakati wote" au "daima zaidi ya nilivyofanya kabla"

Mdomo wangu utaeleza

Mdomo ni njia nyingine ya kumwakilisha mtu mzima. "Nitaeleza" au "Nitazungumza kwa mdomo wangu na kueleza"

haki yako

"jinsi ulivyo mwenye haki" au "vitu vyote vizuri unavyovifanya"

wokovu wako

"jinsi ulivyoniokoa" au "jinsi unavyookoa watu"

ingawa

"hata kama"

Nitakuja

Maana zinazowezekana ni 1) "Nitaenda mahali ambapo watu wanamwabudu Yahwe" au 2) "Nitaenda kwa adui zangu"

kwa matendo makuu ya Bwana Yahwe

Maana zinazowezekana ni 1) "nitawaambia kuhusu matendo makuu aliyoyafanya Bwana Yahwe" au 2) "kwa sababu Bwana Yahwe amenipa nguvu kufanya matendo makuu"

nita taja

"nitazungumzia"

Psalms 71:17

umenifundisha

"umenifundisha vitu vingi"

Mungu, usiniache

"Mungu, tafadhali usiniache"

nimekuwa nikitangaza nguvu yako

"nimekuwa nikiwaambia watu jinsi ulivyo na nguvu"

kwa kizazi kifuatacho

"kwa wale ambao ni watoto leo"

uwezo wako kwa kila mtu atakeyekuja

"na kama ninavyotangaza uwezo wako kwa kila mtu atakayekuja"

kila mtu atakeyekuja

Hii ni kukuza kwa neno. "ili watu wengi niwezavyo kuwaambia wajue"

Psalms 71:19

Haki yako pia, Mungu, iko juu sana

Mwandishi wa zaburi anazungumzia vitu vizuri ambavyo Mungu amefanya kana kwamba viliwekwa pamoja kama jengo kubwa au mlima.

ni nani kama wewe?

Hili ni swali balagha linaloweza kutafsiriwa kama kauli. "hakuna mtu kama wewe!"

taabu saba

"taabu mbaya"

fufua

imarisha au kufanya kuishi tena

kutoka pande za chini ya dunia

"Pande za chini ya dunia" ni sitiari ya mahali ambapo watu huenda wanapokufa. Mwandishi wa zaburi hakuwa amekufa bado, lakini anazungumza kana kwamba alikuwa amekufa. "tunapokaribia kifo"

Psalms 71:21

Na uzidishe ... geuka tena na unifariji

"Nita unizidishie ... nataka ugeuka tena na kunifariji." Tafsiri zingine zinasoma, "Utanizidishia ... utageuka tena na kunifariji"

geuka tena na unifariji

Hii inaeleza tendo moja katika misemo miwili. "nifariji tena"

kwa uaminifu wako

"kwa sababu ninaweza kukutumaini"

nitaimba sifa kwako kwa kinubi, Mtakatifu wa Israeli

"kwako, ambaye ni Mtakatifu wa Israeli, nitaimba sifa huku nikicheza kinubi"

Psalms 71:23

Midomo yangu itapiga kelele ya furaha

"Midomo" ni njia nyingine ya kusema mtu mzima. "Nitapiga kelele ya furaha"

hata nafsi yangu, ambayo umeikomboa

"na nafsi yangu, ambayo umekomboa, itaimba sifa"

nafsi yangu

Hapa "nafsi" inamaanisha mtu mzima"

Ulimi wangu pia utazungumza

Hapa "ulimi" unamaanisha mtu mzima. "nitazungumza pia"

wameaibishwa na kuchanganywa, wale waliotafuta kuniumiza

"wale walio tafuta kuniumiza wameaibishwa na kuchanganywa"

kwa kuwa wameaibishwa na kuchanganywa

"kwa kuwa Mungu amewaaibisha na kuwachanganya"

wale waliotafuta kuniumiza

Hii inamaanisha adui wa mwandishi.

Psalms 72

Psalms 72:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Taarifa ya Jumla:

Maana zinazowezekana kwa ajili ya kichwa cha habari "zaburi ya Sulemani" ni 1) Daudi aliandika zaburi hii kwa ajili ya Sulemani("mwana wa mfalme") au 2) Sulemani (ambaye, kama mwana wa Daudi, alikuwa "mwana wa mfalme") aliandika zaburi hii kama maombi juu yake mwenyewe au 3) mfalme mwingine aliandika kumhusu mwanaye kwa mtindo wa Sulemani. Watu kipindi hicho mara nyingi walijizungumzia kana kwamba walikuwa mtu mwingine. Ingawa, itakuwa vyema zaidi kutafsiri hii kana kwamba mwandishi wa zaburi anamzungumzia mtu mwingine na sio yeye mwenyewe.

Mpe mfalme amri zako za haki, Mungu, haki yako kwa mwana wa mfalme

Maana zinazowezekana ni 1) "Nipe mimi, mfalme, amri zako za haki, Mungu, haki yako kwa mwana wa mfalme" au 2) "Nipe mimi, mfalme, amri zako za haki, Mungu, haki yako kwangu, mwana wa mfalme." Watu kipindi hicho mara nyingi walijizungumzia kana kwamba walikuwa mtu mwingine. Ingawa, itakuwa vyema zaidi kutafsiri hii kana kwamba mwandishi wa zaburi anamzungumzia mtu mwingine na sio yeye mwenyewe.

Mpe mfalme amri zako za haki

"Mwezeshe mfalme kuhukumu kwa haki"

haki yako kwa mwana wa mfalme

"Mwana wa mfalme aweze kutenda yanayokupendeza wewe"

Ahukumu

Kama ni Daudi aliandika hii, anamzungumzia mwana wake, "mwana wa mfalme," anazungumzia wakati ambao mwana wake atakuwa mfalme. Kama ni Sulemani aliyeandika hii, hata kama anaandika kujihusu, itakuwa vyema kuandika kana kwamba anaandika kumhusu mtu mwingine. Vyovyote vile, "mfalme ahukumu" ndio tafsiri bora zaidi.

watu wako ... maskini wako

Mwandishi wa zaburi anazungumza na Mungu.

na maskini wako

"na mfalme awahukumu watu wako maskini"

Milima itoe amani ... na vilima vitoe haki

Mwandishi wa zaburi anazungumzia watu wa Israeli kana kwamba ni milima na vilima ambapo wanaishi. Anazungumzia milima na vilima kana kwamba ni nchi nzima ya Israeli, kana kwamba nchi ni bustani itoayo matunda, na amani na haki kana kwamba ndio matunda. "Watu wa wa nchini waishi kwa amabi ... wafanye kila kitu kwa haki"

Psalms 72:4

awahukumu

Anayezungumziwa hapa ni mtu atakaye hukumu

kumvunja vipande vipande mkandamizaji

"kumwangamiza kabisa yule anayewakandamiza"

wakati jua bado linadumu, na wakati mwezi bado upo

Jua na mwezi ni mfano wa maneno kwa ajili ya mchana na usiku, ambayo pamoja ni maneno ya ujumla kwa ajili ya wakati wote.

Psalms 72:6

Aje chini kama mvua juu ya nyasi zilizofyekwa

Mfalme atakuwa mwema, na atafanya mambo mema kwa watu wake kana kwamba alikuwa mvua ikiifanyia mema nyasi zilizotoka kukatwa."

Aje

"Natamani kwamba aje"

kama mvua zinazomwagia

"Aje chini kama mvua zinazomwagia." Mfalme atakuwa mwema, na atafanya mambo mema kwa watu wake kana kwamba alikuwa mvua ikiifanyia mema ardhi.

mwenye haki

Kivumishi "haki" kinaweza kutafsiriwa kama msemo wa nomino. "mtu mwenye haki"

katika siku zake

Maana zinazowezekana ni 1) "wakati mfalme anatawala" au 2) "maadamu mtu mwenye haki anaishi" au "maadamu watu wenye haki wanaishi"

kuwepo amani tele

Mwandishi wa zaburi anazungumza kana kwamba amani ni kitu cha kugusa kama chakula. "Tele" ni wakati kuna kingi kwa kitu. "watu wenye haki waweze kuishi kwa amani ya kweli"

hadi mwezi usiwepo tena

"maadamu mwezi unang'ara" au "milele"

Psalms 72:8

Awe na mamlaka

"Mfalme awe na mamlaka"

kutoka bahari hadi bahari, na kutoka kwenye mto hadi mwisho wa nchi

Misemo hii miwili inazungumzia mifano miwli ya tofauti ikimaanisha dunia nzima.

kutoka bahari hadi bahari

kutoka bahari ya Chumvi na bahari ya Kinerethi mashariki mwa bahari ya Shamu magharibi.

mto

"mto Frati," ambao Waisraeli walisafari kwenda huko kwa nchi kwa kuelekea kaskazini.

mwisho wa nchi

hadi umbali ambao watu waliweza kusafiri ardhini kwa njia tofauti kufika kusini. Waisraeli walizungumzia dunia kana kwamba ilikuwa tambarare yenye mwisho.

rambe vumbi

Hii ni sitiari ya aibu kubwa. "wanafanye kila wawezacho ili awaruhusu waishi"

Tarshishi

jina la sehemu

onyesha

"toa"

toa zawadi

"onesha zawadi"

Seba

Hili ni jina la nchi. Sio nchi sawa na ile ya Sheba.

Psalms 72:11

wanguke chini mbele yake

"sujudu mbele yake" au "mheshimu yeye kama mfalme wao"

mataifa yote

"watu wanaoishi katika kila taifa"

hana msaidizi mwingine

"hakuna wa kumsaidia"

Psalms 72:13

Anahuruma kwa maskini na wahitaji

"Anataka kuzuia maskini na wahitaji kuhangaika"

maskini na wahitaji

Hapa maneno "maskini" na "wahitaji" yana maana ya kufanana na yanasisitiza kwamba hawawezi kujisaidia wenyewe.

Anaokoa maisha yao

"Anawaokoa" au "Anawakomboa"

ukandamizaji na vurugu

Maneno haya mawili yana maana zinazo fanana na yanasisitiza jinsi wahitaji wanavyohangaika. "wale wanao wakandamiza na kuwaumiza"

damu yao ni ya dhamani machoni pake

"anataka waishi vizuri"

damu yao

"maisha yao" au "hali yao"

machoni pake

"kwake"

Psalms 72:15

Aishi!

"Mfalme aishi muda mrefu!" au "Natamani kwamba mfalme aishi muda mrefu!"

dhahabu ya Sheba ipewe kwake

Hii inaweza kuelezwa kwa njia ya kutenda, "na wampe dhahabu ya Sheba" au "na apokee dhahabu ya Sheba"

siku nzima

"kwa kuendelea"

nafaka tele

"tele" ni wakati kuna wingi wa kitu. "nafaka nyingi" au "nafaka ya kutosha"

mazao

mimea ambayo watu huoteshi kwa ajili ya chakula

tikisike

majani yanaposogea wakati upepo mwepesi unapoyapuliza.

kama Lebanoni

"kama miti ya seda ya Lebanoni." Miti hii ilikuwa mizuri na ilikuwa na mbao iliyo kuwa nzuri kwa ajili ya ujenzi. Maana ya hii inaweza kuwekwa wazi.

watu wastawi katika miji kama nyasi shambani

Mafanikio ya watu mijini yanazungumziwa kana kwamba yalikuwa nyasi zinazoota mashambani.

Psalms 72:17

Jina lake lidumu milele

"Watu wajue kumhusu yeye daima" au "Watu wasisahau kamwe yeye ni nani"

Jina lake

"Jina la mfalme" au "sifa ya mfalme" au "umaarufu wa mfalme"

kama jua

"maadamu jua linang'aa"

watu wabarikwe kwake

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mungu amsababishe kufanya mambo mazuri kwa ajili ya watu"

wamuite aliye barikiwa

"watambue kuwa Mungu amembariki"

Psalms 72:18

Taarifa ya Jumla:

Mistari hii ni zaidi ya mwisho wa zaburi hii. Ni kauli ya kufunga ya kitabu kizima cha 2 cha Zaburi, kinachoaanza Zaburi 42 hadi Zaburi 72.

Yahwe Mungu, Mungu wa Israeli, abarikiwe

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Watu wambariki Yahwe Mungu, Mungu wa Israeli"

Jina lake tukufu libarikiwe milele

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Watu walibariki jina lake tukufu milele" au kufanya "jina" kama namna nyingine ya kusema Yahwe mwenyewe, "watu daima wajue jinsi alivyo mtukufu"

Jina lake tukufu libarikiwe

"yeye aliye mtukufu, abarikiwe"

dunia nzima ijazwe na utukufu wake

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "utukufu wake uijaze dunia yote" au "aijaze dunia yote na utukufu wake"

Amina na Amina

Neno "Amina" linarudiwa kusisitiza kukubali kilichosemwa. "Hakika iwe hivyo"

Maombi ya Daudi mwana wa Yese yanaisha

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Daudi mwana wa Yese amemaliza maombi yake" au "Haya ni maombi ya mwisho ya Daudi mwana wa Yese"

Psalms 73

Psalms 73:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Asafu

"Hii ni zaburi Asafu ambayo aliandika"

miguu yangu kidogo iteleze; miguu yangu kidogo iteleze chini yangu

Mwandishi wa zaburi anazungumzia kushindwa kumwamini Mungu na kutaka kutenda dhambi kama vile kidogo aanguke kwenye njia inayo teleza. "Kidogo niache kumwamini Mungu, kidogo niwe na hatia ya kutenda dhambi kubwa dhidi yake"

niliwaonea wivu wenye kiburi

"sikutaka watu wenye kiburi wawe na vitu vizuri walivyo kuwa navyo"

wenye kiburi

Kivumishi "kiburi" kinaweza kutafsiriwa kama msemo wa nomino. "watu wenye kiburi"

mafanikio ya waovu

Neno "mafanikio" linaweza kutafsiriwa kama kitenzi. "jinsi waovu walivyo na vitu vingi vizuri"

waovu

Kivumishi "waovu" kinaweza kutafsiriwa kama msemo wa nomino. "watu waovu"

Psalms 73:4

Taarifa ya Jumla:

Asafu anaanza kueleza ambavyo wakati mwingine anataka kulalamika kwa Mungu kuhusu wale ambao wana "kiburi" na "waovu".

mizigo ya watu wengine

Neno "mizigo" ni njia nyingine ya kusema mahangaiko ya maisha ya kila siku (hitaji la chakula, pango, nguo, na afya)

hawateswi kama wanaume wengine

"hawateseki kama watu wengine wanavyoteseka"

Psalms 73:6

Taarifa ya Jumla:

Asafu anaendelea kueleza ambavyo wakati mwingine anataka kulalamika kwa Mungu kuhusu wale ambao wana "kiburi" na "waovu".

Kiburi kinawapamba kama mkufu shingoni; vurugu inawavika kama joho

Hii inamaanisha waovu wanawaonesha wote jinsi walivyo na kiburi na vurugu kana kwamba wamevaa mkufu au joho zuri.

mkufu ... joho

Hii inaonesha vitu ambavyo matajiri na watu muhimu huvaa.

mkufu

ni kama mnyororo mdogo uliotengenezwa na madini kama dhahabu ambayo huvaliwa shingoni.

Kutokana na upofu wa hivi huja dhambi

Kwa sababu ni kama watu vipofu ambao hawaoni waendako, wanatenda dhambi bila kujua. Kuwa kipofu ni njia nyingine ya kusema mtu hawezi kuona jinsi alivyo muovu.

mawazo maovu yanapitia mioyoni mwao

Hapa mwandishi wa zaburi anaelezea mawazo ya watu kana kwamba ni watu. Pia anaelezea uhalisia wa ndani wa watu waovu kana kwamba ni majengo ambao wanaweza kutembea humo. "ndani yao huwa wanawaza mambo mengine maovu ya kufanya"

Psalms 73:8

Taarifa ya Ujumla:

Asafu anaendela kueleza ambavyo wakati mwingine anataka kulalamika kwa Mungu kuhusu wale ambao wana "kiburi" na "waovu".

Hudhihaki

Yule ambaye wanamdhihaki inaweza kuelezwa vizuri. "Wanamdhihaki Mungu na watu wake"

Wanaweka mdomo wao dhidi ya mbingu

Hapa neno "mbingu" ni njia nyingine ya kusema Mungu, ambaye anaishi mbinguni. "wanazungumza dhidi ya Mungu aliye mbinguni"

Wanaweka mdomo wao

"kuzungumza vikali" au "kuzungumza na kusudi"

ulimi wao unatembea duniani

Neno "ulimi" ni njia nyingine ya kusema watu wenyewe. Maana zinazowezekana ni 1) "wanaenda duniani wakisema mambo mabaya kumhusu Mungu" au "wanaenda kila mahali na kujisifia."

Psalms 73:10

Taarifa ya Jumla:

Asafu anaendelea kueleza ambavyo wakati mwingine anataka kulalamika kwa Mungu kuhusu wale ambao wana "kiburi" na "waovu"

watu wake wanawageukia

Maana zinazowezekana ni 1) "Watu wa Mungu wanawapenda watu waovu" au "watu waovu wanarudi sehemu hii"

maji mengi yanatolewa

Maana zinazowezekana ni 1) "Watu wa Mungu wanasikiliza kwa furaha maneno ya watu waovu" au 2) "watu waovu wana chakula cha kutosha kula na divai ya kunywa"

Wanasema

watu waovu wanasema

Mungu anajuaje? Kuna ufahamu kwa Aliye juu?

Maswali haya yenye balagha yanaonesha dharau kwa Mungu. Maswali haya yanaweza kutafsiriwa kama kauli. "Hakika Mungu hajui tunalolifanya. Aliye juu hana ufahamu wa hili."

Psalms 73:13

Taarifa ya Jumla:

katika mistari ya 13 na 14, Asafu anaendelea kueleza ambavyo wakati mwingine anataka kulalamika kwa Mungu kuhusu wale ambao wana "kiburi" na "waovu". katika mstari wa 15 anaanza kuzungumza kuhusu kile ambacho anakiwaza kweli.

nime

hapa anayezungumza ni Asafu.

ulinda moyo wangu

Asafu anazungumzia kulinda moyo wake kana kwamba analinda mji au jengo dhidi ya maadui. "nimekuwa na mawazo masafi"

kunawa mikono yako ndani ya pasipokuwa na hatia

Mwandishi anazungumzia usafi kama vile amenawa mikono yake kwa kutokua na hatia badala ya maji. "matendo yangu yamebaki masafi" au "nimenawa mikono yangu kuonehsa kuwa sina hatia"

siku nzima

"wakati wote"

nimeteseka

"uminifanya kuteseka."

kuadhibiwa

"nimepewa adhabu"

Kama ningesema, "nitasema vitu hivi," basi ningekuwa ninasaliti kizazi hiki cha wato wako.

Hii hali ya kubuni haikutokea. "Sijawahi kusema, 'nitasema vitu hivi,' kwa hiyo sikusaliti kizazi hiki cha watoto wako"

Psalms 73:16

vitu hivi

Vitu vizuri vinavyowatokea watu "waovu"

hatima yao

"nini hutokea kwa watu waovu wanapokufa"(UDB) au "watu waovu wanakufa je"

Psalms 73:18

umewaweka

Waliowekwa ni waovu.

sehemu telezi

"ardhi isiyo imara au salama"

Jinsi wanavyokuwa jangwa kwa muda mfupi

Neno "jangwa" ni njia nyingine ya kusema watu waliopoteza kila kitu kizuri. "Jinsi wanavyoangamizwa haraka"

kamandoto baada ya mtu kuamka

Waovu hawatadumu zaidi kama mtu anachoona kwenye ndoto. Inapotea mara tu mtu anapoamka.

Psalms 73:21

moyo wangu ulihuzunika

neno "moyo" ni njia nyingine ya kusema mawazo na hisia za mtu. "nilikuwa na huzuni sana"

niliumia sana

Mwandishi wa zaburi anazungumzia maumivu ya hisia kana kwamba ni maumivu ya mwili. "nilihisi kama mtu ameniumiza kwa kisu au mshale."

mjinga na kukosa utambuzi

Misemo hii miwili ina maana moja na inasisitiza kiasi gani hakujua. "mjinga sana"

kukosa utambuzi

"kutukuelewa kitu"

yako

Hapa anayemaanishwa ni Mungu.

Psalms 73:23

daima niko na wewe

Anayezungumza hapa ni Asafu. Anayezungumziwa ni Mungu.

unanishika mkono wangu wa kuume

hii inaonesha mahusiano ya karibu na Mungu yanayotoa uimara na ulinzi. "unanishika karibu"

kunipokea katika utukufu

Maana zinazowezekana ni 1) "unaniweka mahali ambapo watu wataniheshimu" au 2) "nipe heshima kwa kunipeleka mahali ambapo upo."

Psalms 73:25

Nina nani mbinguni ila wewe?

Unaweza kutafsiri hii kama kauli. "Hakuna mtu mbinguni kwa ajili yangu ila wewe" au "Wewe pekee ndiye niliye naye mbinguni"

mbinguni

mionngoni mwa miungi" au "miongoni mwa viumbe vya ajabu"

hakuna mtu duniani

"hakuna binadamu"

Mwili wangu na moyo wangu

Misemo hii miwili ina maana ya kufanana. Pamoja inamaanisha mtu kamili. "Mwili wangu na akili"

Psalms 73:27

Taarifa ya Jumla:

Asafu anaendelea kumzungumzia Mungu.

Wale walio mbali na wewe

Hapa wazo la kukaa mbali na Mungu linalinganishwa na kutokuwa tayari kumtii. "Wale wasiotaka kukutii"

kimbilio langu

Mwandishi anamzungumzia Yahwe kana kwamba alikuwa sehemu ambayo mtu anaweza kutorokea kwa usalama.

Psalms 74

Psalms 74:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Maschili ya Asafu

Hii ni maschili ambayo Asafu aliandika."

Maschili

Hii inaweza kumaanisha mtindo wa muziki.

Mungu, kwa nini umetukataa milele?

Hii inaweza kutafsiriwa kama kauli. "Mungu, hatujafanya kosa, lakini umetukataa milele!"

Kwa nini hasira yako inawachoma kondoo wa malisho yako?

Hii inaweza kutafsiriwa kama kauli. "Sisi ndio ulio ahidi kututunza, na hatujafanya kosa, lakini sasa una hasira na sisi!"

kondoo wa malisho yako

Asafu anawazungumzia watu wa Israeli kana kwamba ni kondoo. "dhidi ya Israeli, ambao ni kama kondoo unaowalisha kwenye malisho yako"

Kumbuka

"Kuwa makini kwa." Mungu hajasahau watu wake, lakini haonekani kuwafikiria.

urithi wako mwenyewe

"wako milele"

Psalms 74:3

Taarifa ya Jumla:

Mistari hii inaeleza tukio halisi, shambulizi la kimwili lililofanyika katika hekalu la Israeli ndani ya Yerusalemu.

Njoo uone

Asafu anaongea na Mungu, anamuomba aje aangalie uharibifu.

wameunguruma

Maadui walipiga kelele kwa mlio mkubwa wa ushindi.

nakshi

Hii inamaanisha urembo wa kuchonga kwenye mbao, chuma au mawe ya hekaluni.

Psalms 74:7

Taarifa ya Jumla:

Asafu anaendelea kuelezea uharibifu wa hekalu.

waliweka ... walisema ... walichoma

Hapa wanaozungumziwa ni maadui waliotajwa.

walisema mioyoni mwao

Hii ni lahaja. "Wakajiambia" au "wakajiwazia"

Psalms 74:9

Taarifa ya jumla:

Asafu anamueleza Mungu kuhusu uharibifu anaouona.

Hatuoni ishara zingine tena

Maanza zinazowezekana ni 1) "Hatuoni tena ishara za miujiza kutoka kwa Mungu" au 2) "Alama zetu zote takatifu hazipo" au 3) kama kuzungumzia bendera na alama zajeshi, "Jeshi letu limeangamizwa kabisa."

Hadi lini, Mungu, adui atatupa matusi kwako?

Hii inaweza kutafsiriwa kama kauli. "Mungu, adui amekuwa akikurushia matusi kwa muda mrefu sana!"

Adui atakufuru jina lako milele?

Hii inaweza kutafsiriwa kama kauli. "Inaonekana kana kwamba hautamzuia adui kukufuru jina lako!"

atakufuru jina

Neno "jina" ni njia nyingine ya kusema Mungu mwenyewe. "anasema wewe ni mbaya" au "anakutukana"

Kwa nini unazuia mkono wako, mkono wako wa kuume?

Mwandishi wa zaburi anamzungumzia Mungu kana kwamba ana mwili. Hii inaweza kutafsiriwa kama kauli. "Acha kuzuia mkono wako, mkono wako wa kuume!"

unazuia mkono wako

Hapa neno "mokono" ni njia nyingine ya kusema nguvu. "usionesha nguvu yako" au "usitumie nguvu yako kuwaangamiza adui zako"

mkono wako wa kuume

"mkono wako wenye nguvu zaidi"

Toa mkono wako wa kuume kutoka kwenye vazi lako

Mwandishi wa zaburi anamzungumzia Mungu kana kwamba ana mwili. "Acha kuficha nguvu yako na uchukue hatua"

Psalms 74:12

Taarifa ya Jumla:

Hii inaanzisha wazo jipya: Asafu anatangaza ukuu wa matendo ya Mungu katika historia ya watu.

Mungu amekuwa mwema tangu nyakati za zamani

Maana zinazowezekana ni 1) Asafu anazungumza kama mwakilishi wa Israeli, "Mungu amekuwa mfalme wetu tangu Israeli lilipokuwa taifa" au 2) "Mungu, mfalme wangu, alikuwa hai hata katika nyakati za kale."

akileta wokovu

"kuokoa watu"

Uliligawa ... ndani ya maji

Asafu inawezekana anazungumzia wakati ambao Mungu aliitoa Israeli kutoka Misri, akagawa bahari, akawaongoza Waisraeli kwenye nchi kavu, kisha kuzamisha jeshi la Farao.

Uliligawa bahara kwa nguvu yako

Asafu anamzungumzia Mungu kana kwamba ana mwili. "Una nguvu sana uliweza kufanya nchi kavu katikati ya bahari.

bahari

"maji makuu"

uliponda vichwa vya wanyama wakubwa ndani ya maji

Inawezekana Asafu anamzungumzia Farao na jeshi lake kama vile walikuwa wanyama wa baharini. "Ulipoua jeshi la Farao, ilikuwa kama umeponda vichwa vya wanyama wakubwa ndani ya maji"

Psalms 74:14

Taarifa ya jumla:

Asafu anaendelea kuzungumzia kile Mungu alichofanya zamani. Inawezekana anazungumzia wakati Mungu alipoitoa Israeli kutoka Misri na kuangamiza jeshi la Farao baharini.

lewiathani

Lewiathani ni mnyama wa baharini. Inaashiria adui mkatili.

Ulipasua chemchemi na vijito

"Ulisababisha chechemi na vijito kutiririka kutoka kwenye ardhi ngumu iliyo kauka"

Psalms 74:16

Taarifa ya Jumla

Asafu anaendelea kukumbuka nguvu ya ajabu ya Mungu.

mipaka ya dunia

"mipaka ya nchi na bahari"

Psalms 74:18

Taarifa ya Jumla:

Asafu anaomba msaada wa Mungu.

Ita akilini

"Vuta nadhari."

adui alitupa matusi kwako

Asafu anazungumzia maneno ya matusi kana kwamba ni vitu , kama mawe, ambavyo adui alikuwaakitumia kumponda Yahwe. "adui walikutukana mara nyingi"

maisha ya njiwa wako

Asafu anajizungumzia kana kwamba ni njiwa, ndege asiyeweza kujilinda. "mimi, njiwa wako." Msemo huu pia ni sitiari kwa ajili ya watu wa Israeli.

njiwa

Ndege mdogo asiyeweza kujilinda na mara nyingi hutunzwa kama ndege wa kufuga.

mnyama pori

Msemo huu unaweza kuwa ni sitiari kwa ajili ya adui wa Israeli. "adui mkatili ambaye ni kama mnyama pori"

Usisahau maisha ya watu wako walio kandamizwa milele

Usiendelee milele kutokufanya kitu kuwasaidia watu wako walio kandamizwa" "Njoo upesi kuwasaidia watu wako walio kandamizwa"

Psalms 74:20

Taarifa ya Jumla:

Asafu anaendela kuomboleza kwa Yahwe.

sehemu zenye giza za nchi zimejaa sehemu za vurugu

Asafu anazungumzia "sehemu" kana kwamba ni chombo ambamo mtu anaweza kuweka "sehemu za vurugu." "watu wenye vurugu wanafanya matendo maovu katika sehemu za giza nchini pale wanapoweza"

sehemu zenye giza za nchi

Neno "giza" linaweza kuwa ni sitiari ya sehemu ambapo mambo mabaya yanatokea au nchi ambazo Waisraeli walipelekwa katika uhamisho.

Usiwaache walio kandamizwa warudi na aibu

"Usiwaache watu waovu wawashinde walio kandamizwa na kuwaaibisha"

walio kandamizwa

Hawa ni watu wanaotendewa ukatili na watu wenye nguvu.

maskini na walio kandamizwa

Maneno "maskini" na "walio kandamizwa" yanamaanisha kitu kimoja na yanasisitiza kuwa Yahwe anawaokoa wengi wanaohitaji msaada wake.

Psalms 74:22

tetea heshima yako mwenyewe

"onesha kila mtu kuwa uko sawa"

ita akilini

"Vuta nadhari." Mungu hajasahau jinsi wapumbavu wanavyomtukanu, lakini haonekani kuwa anafikiria hilo.

sauti ya adui zako

Neno "sauti" ni njia nyingine ya kusema maneno ambayo watu wanatumia wakati wakizungumza. "kile ambacho adui zako wanasema"

au ghasia ya wale wanaoendelea kukaidi

Mwandishi wa zaburi anazungumzia maneno ya wale wanaomkaidi Mungu kana kwamba yalikuwa na sauti kubwa ya wanyama au vitu ambavyo havina uhai kama maji au upepo. "na vuta nadhari kwa sauti kubwa na maneno yasiyo kuwa na maana ya wale wanao endelea kukukaidi"

kukaidi

kupinga kwa nguvu

Psalms 75

Psalms 75:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Taarifa ya Jumla:

Watu wa Mungu wanazungumza katika 75:1, na Mungu anazungumza katika 75:2-3.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

weka katika Al Tashhethi

Hii inaweza kuwa inamaanisha mtindo wa muziki.

Zaburi ya Asafu

"Hii ni zaburi ambayo Asafu aliandika"

wakazi wote

"watu wote wanaosishi ndani yake"

ninazifanya imara nguzo za dunia

"ninaiweka dunia kutoangamizwa" au "waweke watu wangu salama"

Sela

Hili linaweza kuwa neno la kimuziki linalowaongoza watu jinsi ya kuimba au kujecheza vyombo hapa. Tafsiri zingine huandika neno hili la Kiebrania, na zingine haziliweki.

Psalms 75:4

Nilisema

Maana zinazowezekana ni 1) Mungu anazungumza au 2) Asafu anazungumza

Msiwe na kiburi ...Msiinue ... Msiinue ... msizungumze

Anaye zungumza anazungumza na watu wengi waovu.

na kwa waovu

"na nikasema kwa waovu"

Msiinue juu pembe

Asafu anazungumzia watu waovu kana kwamba ni wanyama wenye pembe vichwani mwao, wanonyosha shingo zao na kuweka vichwa vyao juu kutisha wanyama wengine. "Msiwe wajasiri" au "Msijivune jinsi mlivyo na nguvu"

Msiinue pembe yenu juu

Asafu anazungumzia watu waovu kana kwamba ni wanyama wenye pembe vichwani mwao, wanonyosha shingo zao na kuweka vichwa vyao juu kutisha wanyama wengine. "Kuweni waangalifu sana kutokuwa na majivuno kuwa mko bora zaidi ya Mungu"

na shingo yenye jeuri

Asafu anazungumzia watu waovu wanaomkaidi au kupingana na Mungu kana kwamba ni wanyama wenye pembe vichwani mwao, wanonyosha shingo zao na kuweka vichwa vyao juu kutisha wanyama wengine. "kwa kiburi"

Sio mashariki ... kuinuka kunakotokea

Asafu anamzungumzia yule anayeinua kana kwamba ndio tendo la kuinua. Anazungumzia pia Mungu kumpa nguvu na heshima mtu kana kwamba Mungu alikuwa akimnyanyua mtu kimwili. "Yule ambaye atakuinua hatakuwa mtu atokaye mashariki" au "Yule ambaye atakufanya kuwa na nguvu na kuwafanya watu wakuheshimu hatakuwa mtu anayetoka mashariki"

Psalms 75:7

Taarifa ya Jumla:

Asafu anamzungumzia Mungu.

huleta chini na huinua juu

"huwashusha watu wengine na kuwainua watu wengine." Maneno "huleta chini" na "huinua juu" ni sitiari ya Mungu kuwapa nguvu watu na kuchukua nguvu yao. "humfanya mtu mmoja mfalme katika nafasi ya mwingine" au "huondoa nguvu ya mtu mmoja na kumpa nguvu mtu mwingine"

kikombe cha divai ya povu ... imechanganywa na vikolezo

Yahwe anapowaadhibu watu watakuwa kama watu waliokunywa divai kali na kuugua.

divai ya povu

Povu ni sitiari ya nguvu ya divai kuwafanya watu walewe. "divai kali"

vikolezo

majani yaliyo kaushwa au mbegu za ardhini

kuimwaga nje

kuimwaga kutoka kwenye chombo kikubwa hadi kwenye vikombe ambavyo watu watatumia kunywa

watainya hadi tone la mwisho

"kunywa kila tone lake"

Psalms 75:9

Anasema

Mungu anasema

nitakata pembe zote za

Pembe za mnyama ni sitiari ya nguvu ya mtu. "ondoa nguvu yote kutoka kwa"

pembe za mwenye haki zitainuliwa juu

Pembe za mnyama ni sitiari ya nguvu ya mtu. "nitainua pembe za mwenye haki" au "nitamfanya mwenye haki kuwa na nguvu"

Psalms 76

Psalms 76:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

kwenye vyombo vya nyuzi

"watu wanapaswa kucheza vyombo vya nyuzi na wimbo huu"

Zaburi ya Asafu

"Hii ni zaburi ambayo asafu aliandika"

amejifanya kujulikana katika Yuda

"amesababisha watu wa yuda kujua yeye ni nani" au "amejifanya kuwa maarafu katika Yuda"

jina lake ni kuu katika Israeli

Maneno "jina lake" ni njia nyingine ya kusema sifa yake. "watu wa Israeli wanamwona kuwa mwema na mwenye nguvu"

sehemu yake ya kuishi

"sehemu aliyochagua kuishi"

Huko alivunja mishale ya upinde, ngao, upanga, na silaha zingine za vita

Maneno haya yanaweza kuwa ni sitiari ya Mungu kuwasababisha watu wa Yuda kuishi katika amani bila ya kuwa na hofu ya adui zao kufanya vita dhidi yao.

Sela

Hili linaweza kuwa neno la kimuziki linalowaongoza watu jinsi ya kuimba au kujecheza vyombo hapa. Tafsiri zingine huandika neno hili la Kiebrania, na zingine haziliweki.

Psalms 76:4

Taarifa ya Jumla:

Asafu anamzungumzia Mungu kana kwamba Mungu alikuwa askari anayerudi kutoka katika mlima baada ya kushinda vita vikuu.

Unang'aa kwa nguvu na kuonesha utukufu wako

Mseno wa pili unaimarisha ule msemo wa kwanza ya kwamba utukufu wa Yahwe inaonesha Yahwe kung'aa kwa nguvu.

Unang'aa kwa nguvu

Maneno "unang'aa kwa nguvu" ni sitiari kwa ajili ya kuwa mkuu. "Unaonesha jinsi ulivyo mkuu"

wenye mioyo ya ujasiri walitekwa

"Watu wako waliwaua askari shupavu wa adui zao na kuchukua mali zao zote"

walisinzia

Hapa "walisinzia" ni tasifida ya kufa. "walikufa' au "walianguka chini na kufa"

Psalms 76:6

Kwa kukemea kwako

"Ulipowakemea"

walisinzia

"walikufa" au "walianguka chini na kufa"

nani anaweza kusimama mbele ya macho yako unapokuwa na hasira?

"Hakuna mtu anayeweza kusimama machoni pako unapokuwa na hasira" au "Unaweza kumwangamiza yeyote ambaye una hasira naye"

Psalms 76:8

ulifanya hukumu yako isikike

"ulitangaza hukumu" au "ulitangaza jinsi ambavyo ungeenda kuwaadhibu watu waovu"

dunia ili...

Hapa "dunia" ni njia nyingine ya kusema watu wanaoishi duniani. "watu wa duniani"

kutekeleza hukumu

"kupitisha hukumu" au "kuwaadhibu watu waovu"

Sela

Hili linaweza kuwa neno la kimuziki linalowaongoza watu jinsi ya kuimba au kujecheza vyombo hapa. Tafsiri zingine huandika neno hili la Kiebrania, na zingine haziliweki.

Psalms 76:10

Hakika

"Hakika" inaeleza matarajio ya kwamba kinachofuata lazima kitatokea.

hukumu yako ya hasira dhidi ya wanadamu italeta sifa kwako

Maana zinazowezekana ni 1) "watu watakusifu kwa sababu una hasira na waovu na una wahukumu" au 2) "watu ambao wana hasira na wewe watafanya vitu vitakavyo sababisha watu wakusifi wewe"

unijifungwa na kile kilichobaki katika hasira yako

Hasira ya Yahwe inazungumziwa kama kitu ambacho anaweza kujifunga kama mshipi. "unajifunga kama mshipi hasira yako iliyobaki"

Psalms 76:11

kwake ambaye anapaswa kuogopwa

"Yahwe, ambaye wanapaswa kumwogopa"

Huzikata roho za wakuu

Msemo "Huzikata roho" ni lahaja inayomaanisha kuwa huvunja roho au huzinyenyekesha. "Huwanyenyekesha wakuu"

anaogopwa na wafalme wa duniani

"wafalme wa duniani wanamwogopa"

Psalms 77

Psalms 77:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Yeduthuni

Mmoja wa wanamuziki wakuu wa Daudi alikuwa na jina hili. Hii inaweza kuwa inamaanisha ni yeye.

Zaburi ya Asafu

"Hii ni zaburi ambayo Asafu aliandika"

Psalms 77:2

nilinyosha mikono yangu

"niliomba na mikono yangu ikiwa imenyoshwa"

Nafsi yangu ilikataa kufarijiwa

"Nafsi" ni njia nyingine ya kusema mtu. "Sikumruhusu yeyote kujaribu kunifariji"

Nilimuwaza Mungu na nikagumia; Nilimuwaza huku nikiishiwa nguvu

Misemo hii miwili ina maana za kufanana na inaunganishwa kwa ajili ya mkazo.

huku nikiishiwa nguvu

"wakati nafsi yangu ikiishiwa nguvu" au "wakati nafsi yangu ilipolemewa"

Sela

Hili linaweza kuwa neno la kimuziki linalowaongoza watu jinsi ya kuimba au kujecheza vyombo hapa. Tafsiri zingine huandika neno hili la Kiebrania, na zingine haziliweki.

Psalms 77:4

Taarifa ya jumla:

Baada ya kuzungumza na Mungu, Asafu anazungmza na Mungu katika mstari wa 4 na kisha anarudi kusungumza kuhusu Mungu.

Uliyashika macho yangu wazi

"Nilisema kwa Mungu, 'Ulishika macho yangu wazi.'"

Uliyashika macho yangu wazi

Macho yaliyowazi ni njia nyingine ya kusema kushindwa kulala. "ulinizuia kulala"

siku za kale, kuhusu siku za zamani

"kuhusu vitu vilivyotokea siku za zamani sana"

Psalms 77:6

Nikaita akilini

Hii ni lahaja ya kukumbuka. "Nilikumbuka"

kilichotokea

Maana nyingine inayowezekana ni "nini kilikuwa kinatokea."

Je! Bwana atanikataa milele? Hatanionesha tena fadhila?

Misemo hii miwili inaeleza hisia ya kukataliwa na Bwana.

Hatanionesha tena fadhila

"kufanya vitu ambavyo vinaonesha kuwa amefurahishwa na mimi"

Psalms 77:8

Taarifa ya Jumla:

Kwa sababu Asafu hakuwa na uhakika ya jibu la maswali haya, inawezekana kuwa yalikuwa maswali halisi.

uaminifu wa agano

Katika kuzungumzia "uaminifu wa agano" wa yahwe, daudi anamtumaini Yahwe kuwa aampenda daima. "upendo wa uaminifu"

Je! Wokovu wake ulizima huruma yake

Asafu anazungumzia hasira kana kwamba ni mtu aanayefunga mlango kumzuia mtu mwingine au huruma kutoka nje. "Je! Mungu aliacha kutuonesha huruma kwa sababu ana hasira na sisi"

Psalms 77:10

Nilisema

Maana zinazowezekana ni 1) mwandishi wa zaburi alikuwa akijizungumzia mwenyewe au 2) mwandishi wa zaburi alikuwa akimzungumzia Yahwe.

kubadilika kwa mkono wa kuume wa Aliye juu kwetu

"Mkono wa kuume" ni njia nyingine ya kusema, uwezo, mamlaka au nguvu. "Aliye juu hatumii tena nguvu yake kutusaidia"

Psalms 77:11

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaanza kuzungumza na Yahwe.

ita akilini

"kumbuka"

matendo yako makuu ya kale

"mambo ya ajabu uliyofanya zamani"

Nitatafakari matendo na nitayakumbuka

Misemo hii miwli inaeleza wazo la kutafakari juu ya kile ambacho Yahwe ametenda.

Nitatafakari

"kuwaza kwa kina kuhusu"

nitayakumbuka

"kuwaza yanacho maanisha"

Psalms 77:13

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaendelea kuzungumza na Yahwe.

mungu gani analinganishwa na Mungu wetu mkuu?

"hakuna mungu anayelinganishwa na Mungu wetu mkuu."

onesha nguvu yako katikati ya watu

"onesha watu kutoka makundi mengi ya watu jinsi ulivyo mkuu"

uliwapa watu wako ushindi ... uzao

"ulitupa sisi, wato wako, ushindi ... sisi tulio uzao"

uliwapa watu wako ushindi

"uliwawezesha watu wako kuwashinda adui zao"

uzao wa Yakobo na Yusufu

Hii inamaanisha taifa zima la Israeli.

Psalms 77:16

Maji yalikuona ... yaliogopa ... vilindi vilitetemeka

Asafu anazungumzia maji kana kwamba ni mtu aliyeona kitu kilichomtisha.

Maji yalikuona, na yakaogopa; vilindi vilitetemeka

"maji" na "vilindi" zinamaanisha miili mikubwa ya maji kama bahari.

vilindi

"maji ya kina kirefu zaidi"

Mawingu yalimwaga chini maji

Asafu anazungumzia mawingu kana kwamba ni watu wanamwaga maji kutoka kwenye chombo. "Mvua nyingi ilianguka" au "Ilinyesha kwa nguvu sana"

mishale yako ilitapakaa

Hii ni sitiari inayoelezea radi kama mshale wa Mungu. "radi uliyotengeneza ilitoa mwanga kama mishale"

ilitapakaa

Mishale ilipaa hovyo ovyo.

Psalms 77:18

Sauti yako ya radi

Hii ni kuipa sifa ya mtu, sauti ya radi ya Mungu. "sauti, ambayo ilikuwa na sauti zaidi ya radi" au "sauti kubwa sana"

radi ilimulika ulimwengu

Radi ilionekana kama kuimulika dunia yote. "radi ilimulika kila kitu hadi mwisho wa upeo wa macho"

Njia yako ... njia yako

Misemo hii miwili inamaana za kufanana na imeunganishwa kwa ajili ya mkazo.

nyayo zako

Asafu anamzungumzia Yahwe kana kwamba Yahwe alikuwa ni mtu mwenye miguu.

nyayo zako hazikuonekana

"hakuna mtu aliyeona nyayo zako"

Uliwaongoza watu wako kama kundi

Tashbihi hii inawafananisha watu wa Mungu na kundi la wanyama.

kwa mkono wa

Msemo "kwa mkono" hapa unamaanisha "kwa matendo ya" au "kupitia matendo ya."

mkono

Hapa "mkono" ni njia nyingine ya kusema mtu mzima.

Psalms 78

Psalms 78:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Maschili ya Asafu

"Hii ni maschili ambayo Asafu aliandika."

Maschili

Hii inaweza kumaanisha mtindo wa muziki.

mafundisho yangu

"mimi ninapokufunza"

maneno ya mdomo wangu

Neno "mdomo" ni njia nyingine ya kusema mtu anayezungumza kwao.

fungua mdomo wangu kwa mafumbo

"fungua mdomo wangu na useme mafumbo"

kuimba kuhusu

"sema"

vitu vilivyojificha

mafumbo

Psalms 78:3

Taarifa ya Jumla:

Mstari wa 3 unaendeleza sentensi ya mstari wa 2.

Hatutawatenga na uzao wao

"Hakika tutawaambia uzao wetu kuyahusu"

matendo ya kusifu ya Yahwe

"vitu ambavyo tunamsifia Yahwe"

Psalms 78:5

aliweka

Yahwe aliweka"

amri za agano

Maana zingine zinazowezzekana ni "shuhuda" au "sheria."

Psalms 78:7

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anazungumzia "watoto" wa 78:5.

Psalms 78:9

Waefraimu ... siku ya vita

Hii inawezekana ni sitiari ya kutokutunza agano (mstari wa 10).

Waefraimu

"askari wa Efraimu"

walikuwa na pinde

Inawezekana kuwa askari walikuwa na mishale. "walikuwa na pinde na mishale kwa ajili ya silaha"

Psalms 78:12

nchi ya Sayuni

Hii inamaanisha eneo lililozunguka mji wa Soani, ambao ulikuwa Misri.

Psalms 78:15

Aligawanya

"Mungu aligawanya"

ya kutosha kujaza vilindi vya bahari

"maji zaidi ya walivyoweza kunywa"

mikondo

mito midogo

Psalms 78:17

Walimjaribu Mungu

Walimtaka Mungu kuthibitisha kuwa aliweza kufanya alichosema atafanya kabla ya kumwamini.

mioyoni mwao

"kwa mioyo yao yote"

kuridhisha hamu zao

"ili wale kiasi walichotaka"

Psalms 78:19

Walizungumza

Waisraeli walizungumza

Kweli Mungu anaweza kuandaa meza kwa ajili yetu nyikani?

"Hatuamini kuwa kweli Mungu anaweza kuandaa meza kwa ajili yetu nyikani!" au "Mungu, jithibitishe kwetu kuwa kweli unaweza kuandaa meza kwa ajili yetu nyikani!"

kuandaa meza

"kutupa chakula"

maji yalitoka nje

maji mengi yalitoka haraka

Lakini anaweza kutupa mkate pia? Atatoa nyama kwa ajiil ya watu wake?

Watu wanamcheka Mungu kumtukana kwa maswali haya. "Lakini hatuta amini kuwa anaweza kutupa mkate pia au kutoa nyama kwa ajili ya watu wake hadi tumwone akifanya."

mkate ... nyama

chakula kutoka katika mimea au chakula kutoka katika wanyama. Ingawa hii neno moja linalojumuisha aina zote za chakula.

Psalms 78:21

hasira yake ilishambulia Israeli

"kwa kuwa alikuwa na hasira, alivamia Israeli"

hawakutumaini katika wokovu wake

"hawakumtumaini kuwaokoa"

Psalms 78:23

aliamuru anga

Asafu anazungumzia anga kana kwamba ilikuwa ni mtu anayeweza kusikia na kutii amri za Mungu. "alizungumza na anga'

anga

Maana zinazowezekana ni 1) "anga" au 2) "mawingu."

kufungua mzlango ya anga

Asafu anazungumzia anga kana kwamba ni ghala lenye mzlango. "kufungua anga kana kwamba ni ghala"

Aliwanyeshea mana kwa ajili yao kula, na kuwapa nafaka kutoka mbinguni

Mistari hii miwili inazungumzia tukio moja.

Aliwanyeshea mana

"Alisababisha mana kudondoka kutoka angani kama mvua"

mkate wa malaika

Hii inazungumzia mana. "aina moja ya chakula ambayo malaika hula"

chakula cha kutosha

"kiasi kikubwa cha chakula"

Psalms 78:26

Alisababisha

"Mungu alisababisha"

Aliwanyeshea nyama kama vumbi

"Alisababisha nyama kudondoka kutoka angani kama mvua, na ilikuwepo nyingi sana hadi ilifunika ardhi kama vumbi"

nyama

ndege

kama vumbi... wengi kama mchanga wa baharini

Kulikuwa na ndege zaidi ya ambavyo mtu angeweza kuhesabu.

Psalms 78:29

tamani

"kuwa shauku sana"

Psalms 78:31

Kisha

wakati chakula kilikuwa bado midomoni mwao (78:29)

hasira ya Mungu ikawashambulia

"Mungu alikuwa na hasira na akawashambulia."

akawaleta chini

"akawaua"

hawakuamini matendo yake ya ajabu

Neno "matendo" ni njia nyingine ya kusema Mungu, ambaye alifanya hayo matendo. "hawakuamini kuwa atawatunza licha ya kufanya mambo ya ajabu hivyo"

Psalms 78:33

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaendelea kueleza kile ambacho Mungu alitenda kwa Waisraeli.

alipunguza siku zao kuwa fupi

"aliwaua wakati bado wako wachanga"

miaka yao ilijaa na hofu

Asafu anazungumzia miaka kana kwamba ilikuwa ni vyombo. "mwaka baada ya mwaka walikuwa wakiogopa kila wakati"

kumtafuta

kumwomba walichohitaji afanye ili awalinde

alipowaumiza, walianza ... walirudi na kumtafuta

Hawa ni watu tofauti ambao Mungu "alipunguza siku zao". Baadhi yao walipokufa, wengine walianza "kumtafuta" Mungu.

walirudi

"walitubu" au "walijuta kweli kwa sababu ya dhambi zao"

kwa bidii

"kwa haraka" au "kadri ya uwezo wao"

Psalms 78:35

Taarifa ya Jumla:

Hii inaelezea kile ambacho Waisraeli walichofanya.

ita akilini

"kumbuka"

Mungu alikuwa mwamba wao

Mwandishi anamzungumzia Mungu kana kwamba alikuwa kilima au mlima ambapo watu walienda ili kuwa salama kutoka kwa adui zao. "Mungu ndiye aliyewalinda"

mkombozi wao

"yule aliyewakomboa"

walijipendekeza kwake

"walimwambia kuwa ni wa ajabu wakati hawakuamini hivyo"

kwa midomo yao

Neno "mdomo" ni njia nyingine ya kusema maneno waliyozungumza kwa midomo yao.

mioyo yao haikuwa thabiti kwake

"hawakumtumaini" au "hawakuwa waminifu kwake"

Psalms 78:38

alisamehe udhalimu wao

"aliwasamehe ingawa walifanya matendo maovu"

alizuia hasira yake

Asafu anazungumzia hasira ya Mungu kana kwamba ni mtu mwenye hasira ambaye Mungu alimzuia kushambulia yule aliyemkasirisha. "hakuwaadhibu ingawa alikuwa amekasirishwa nao"

hakutikisa gadhabu yake yote

Asafu anazungumzia gadhabu ya Mungu kana kwamba ni mtu aliyelala ambaye Mungu alimruhusu kulala na hakumwamsha. "hakujiruhusu kuwakasirikia kabisa"

Psalms 78:39

Aliita akilini

"Alikumbuka"

wameumbwa kwa nyama

Neno "nyama," ambalo ni dhaifu halafu hufa, ni njia nyingine ya kusema udhaifu na mauti. "Waisraeli walikuwa wanyonge na siku moja watakufa"

maeneo yenye ukame

"sehemu ambapo hakuna kitu kinachoota"

walimpinga Mungu

Walitaka Mungu kuthibitisha kuwa anaweza kufanya alichosema atafanya kabla hawajamwamini.

Psalms 78:42

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anazungumzia jinsi Mungu alivyowaokoa Waisraeli.

Soani

mji ndani ya Misri

Psalms 78:44

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaeleza alichokifanya Mungu.

makundi ya inzi

inzi wengi sana hadi ikaonekana kama wingu

yaliyo wameza

Inzi ziliwafanya Wamisri wakoswe furaha kama ambavyo wangekuwa kama zingewala Wamisri.

Akawapa panzi mazao yao na kazi yao kwa nzige

"Aliwaruhusu panzi kula mazao yao yote na kuwaruhusu nzige kula kila kitu walichofanyia kazi kupata"

enea

"walitanda kila mahali"

panzi

mdudu anayekula mimea mwenye miguu mirefu anayotumia kwa ajili ya kuruka

Aliwapa panzi mazao yao

Asafu anazungumzia mimea kama zawadi ambayo Mungu aliwapa panzi. "Aliwaruhusu panzi kula mimea yao"

kazi yao kwa nzige

"Aliwapa kazi yao kwa nzige." Asafu anazungumzia kazi ya watu kana kwamba ni zawadi ambayo Mungu aliwapa panzi. Neno "kazi" ni njia nyingine ya kusema mazao ambayo kazi yao ilipata. "Aliwaruhusu nzige kula mazao waliyofanyia kazi kupata"

Psalms 78:47

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaendelea kuelezea kile ambacho Mungu alichofanya kwa Wamisri.

mkuyu

mti unaotoa matunda

miale ya radi

radi yenye ngurumo kubwa

Alinyeshea mvua ya mawe

"Alileta mvua ya mawe" au "Alisababisha mvua ya mawe kuanguka"

Ukali wa hasira yake uliwapiga

Asafu anazungumzia ukali kana kwamba ni mtu anayeweza kumvamia mtu mwingine. "Alikuwa na hasira nao, kwa hiyo aliwashambulia ghafla na kwa ukali"

Ukali wa hasira yake

"Hasira yake kali"

uliwapiga

"aliwavamia wakati hawakuwa wakitegemea chochote kutokea"

Alituma hasira, gadhabu, na taabu kama wakala wanaoleta maafa

Asafu anazungumzia hasira, gadhabu, na taabu kana kwamba ni watu ambao Mungu anaweza kuwatuma kufanya kazi yake. Alikuwa na hasira sana hadi alitaka kuwadhuru Wamisri, kwa hiyo aliwafanyia taabu na kuwapeleka katika maafa"

gadhabu

hasira inayomfanya mtu kutaka kuwadhuru wengine

Psalms 78:50

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaendelea kuelezea kile ambacho Mungu alifanya kwa Wamisri.

Akasambaza njia kwa ajili ya hasira yake

Mwandishi wa zaburi anazungumzia hasira yake kana kwamba ni mtu anayeweza kumtazama Yahwe akijiandaa kuwaadhibu watu kana kwamba alikuwa akitengeneza barabara kwa ajili ya mtu kutembelea. "Alikuwa na hasira sana hadi alifanya yote awezayo kuwadhuru" au "Ilikuwa kana kwamba hasira yake ni jeshi na akalitengenezea barabara kwa ajili ya kutembelea"

hakuwaepusha na mauti

"hakuwaepusha Wamisri na kifo" au "hakuwaruhusu Wamisri kuishi"

aliwapa kwa mapigo

Asafu anazungumzia pigo kana kwamba ni mtu amabye alikuwa anaenda kuwadhuru Wamisri. "aliwafanya wote kuugua sana kwa pigo"

mzaliwa wa kwanza wa nguvu yao

"wanaume wao wa muhimu na bora zaidi"

katika mahema ya Hamu

"miongoni mwa familia za Misiri"

Psalms 78:52

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaendelea kuelezea kile ambacho Mungu alifanya kwa watu wa Israeli.

kama kondoo ... kama kundi

Mwandishi anawazungumzia Waisraeli kana kwamba walikuwa kondoo. Hii inamaanisha kuwa Mungu aliwajali na kuwalinda watu kama mchungaji anavyofanya kondoo wake.

liliwalemea

"wafunika kabisa"

Psalms 78:54

Taarifa ya Jumla

Mwandishi anaendelea kuelezea kile ambacho Mungu alifanya kwa watu wa Israeli.

mkono wake wa kuume ulipata

Maneno "mkono wa kuume" ni njia nyingine ya kusema uweso. "alijishindia kwa kutumia uwezo wake mwenyewe"

akawagawia urithi wao

Maana zinazowezekana ni 1) Mungu aliwapangia Waisraeli urithi wao katika nchi ambayo mataifa mengine yaliwahi kuishi au 2) Mungu aliyapangia mataifa aliyoyaondoa urithi sehemu nyingine. "aliwapa nchi ambayo itakuwa yao daima"

katika mahema yao

Maana zinazowezekana ni 1) aliweka Israeli katika mahema yao wenyewekatika nchi au 2) aliwaweka Israeli katika mahema ambamo aliwaondoa mataifa mengine. "Mahema" mengi haya yalikuwa nyumba kabisa, wakati mataifa mengine yalipoishimo na Waisraeli walipoishimo.

Psalms 78:56

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaendelea kuelezea kile ambacho Mungu alifanya kwa watu wa Israeli.

walipingana na kukaidi

Maneno haya yana maana ya kukaribiana. Mwandishi anayatumia yote kusisitiza kuwa Waisraeli hawakuamini kuwa Mungu atawap mahitaji au kuadhibu maovu kama alivyosema atafanya.

walipingana

Walitaka Mungu kuthibitisha kuwa anaweza kufanya kama alivyosema kabla hajamwamini.

kukaidi

"kataa kutii"

Hawakuwa waaminifu na kutenda kwa uongo

Maneno haya yana maana ya kukaribiana. Mwandishi anayatumia yote mawili kusisitiza kuwa Waisraeli hawakumfanyia Mungu walichosema watafanya.

Psalms 78:58

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaendelea kuelezea kile ambacho Mungu alifanya kwa watu wa Israeli.

walimkasirisha na sehemu zao za juu na kumchokoza na wivu wa hasira kwa sanamu zao

Misemo hii miwli ina maana za kukaribiana.

Psalms 78:60

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaendelea kuelezea kile ambacho Mungu alifanya kwa watu wa Israeli.

Aliruhusu nguvu yake kushikwa na kuwapa adui utukufu wake katika mkono wao

Asafu anazungumzia nguvu ya Mungu na utukufu wake kana kwamba zilikuwa vitu ambavyo watu waliweza kushika na kubeba. Maneno "nguvu" na "utukufu" inawezekana kuwa ni njia nyingine ya kusema sanduku la agano. Neno "mkono" ni njia nyingine ya kusema uwezo wa adui. "aliwaruhusu adui zake kulishika sanduku tukufu la agano lake; aliwapa ili wafanye nalo walichotaka"

Psalms 78:62

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaendelea kuelezea kile ambacho Mungu alifanya kwa watu wa Israeli.

Aliwatoa watu wake kwa upanga

Asafu anawazungumzia watu wa Mungu kana kwamba walikuwa kitu kidogo.

alikasirishwa na urithi wake

"alikasirishwa na watu aliosema watakuwa wake milele"

Moto uliwameza vijana

Maana zinazowezekana ni 1) "Adui walitumia moto kuwaua vijana wao wote" au 2) "Vijana wao walikufa upesi vitani kama moto unavyochoma majani yaliyokauka."

wameza

"Kumeza" ni kula kila kitu haraka.

arusi

sherehe wakati watu wakioa

Psalms 78:64

makuhani walianguka kwa upanga

"adui waliua makuhani wengi wa Israeli kwa kutumia upanga"

wajane wao walishndwa kulia

Maana zinazowezekana ni 1) mtu aliwalazimisha wajane kutolia au 2) makuhani wengi sana walikufa hadi hakukuwa na mazishi sahihi.

wajane

wanawake ambao waume wao wamekufa

Bwana aliamka kama mtu kutoka usingizini

"ilikuwa kana kwamba Bwana aliamka kutoka usingizini"

kama shujaa anayepiga kelele kwa sababu ya mvinyo

Maana zinazowezekana ni 1) kama shujaa aliyekunywa mvinyo mwingi na akawa na hasira kwa sababu aliamshwa na kwa hio alitaka kupigana au 2) kama shujaa aliyekunywa sana mvinyo na sasa anaweza kufikiri na kupigana vizuri kwa sababu amelala.

Psalms 78:67

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaendelea kuelezea kile ambacho Mungu alifanya kwa watu wa Israeli.

hema la Yusufu

"uzao wa Yusufu"

Yusufu ... Efraimu

Efraimu alikuwa mwana wa Yusufu.

Yuda ... mlima Sayuni

Mlima Sayuni ulikuwa katika nchi ambayo kabila la Yuda lilikuwa.

kama mbingu

"juu, kama mbingu"

kama dunia

"thabiti na imara, kama dunia"

Psalms 78:70

taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaendelea kuelezea kile ambacho Mungu alifanya.

kutoka katika mazizi ya kondoo

"kutoka mahali ambapo alikuwa akifanya kazi katika mazizi ya kondoo"

mazizi ya kondoo

nafasi zenye kuta ambapo kondoo hutunzwa

kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na israeli, urithi wake

Neno "mchungaji" ni sitiari ya yule anayewaongoza na kuwalinda watu wengine. "kuwaongoza na kuwalinda uzao wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake"

urithi wake

"wale aliowachagua kuwa wake milele"

Daudi aliwachunga

Neno "mchungaji" ni sitiari ya kuongoza na kulinda. "Daudi aliwaongoza na kuwalinda"

Psalms 79

Psalms 79:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Asafu

"Hii ni zaburi ambayo Asafu aliandika"

urithi wako

"nchi ilikuwa iwe yako milele"

Wamemwaga damu yao kama maji

Neno "damu" ni njia nyingine ya kusemamtu asiye na hatia. Kumwaga damu ni kuua watu wasio na hatia. Watu wengi waliona damu kila siku, kwa hiyo kwa damu kuwa ya kawaida kama maji, watu wengi wa hatia ilibidi wafe. "Wamewaua watu wengi sana wasio na hatia hadi damu iko kila sehemu, kama maji baada ya kunyesha"

hakuwepo wa kuwazika

"hakuna wa kuwazika walio kufa"

Psalms 79:4

Tumekuwa chukizo kwa jirani zetu, kejeli na dhihaka kwa wale waliotuzunguka

Maneno "chukizo," "kejeli," na "dhihaka" ni njia zingine za kusema watu ambao wanachukiza, kejeli, na kudhihaki. "Tumekuwa watu ambao jirani zetu wanatuchukia; wale waliotuzunguka wanatukejeli na kutudhihaki"

Tumekuwa

Wanaozungumziwa ni watu wa Mungu.

dhihaka

kicheko kikubwa cha kumwaibisha mtu

Hadi lini wivu wako wa hasira utawaka kama moto?

"Inaonekana kana kwamba wivu wako wa hasira hautaacha kuwaka kama moto"

wivu wako wa hasira utawaka

Maneno "wivu wako wa hasira" unazungumzia kuwa na wivu na hasira. "utakuwa na wivu na hasira"

utawaka kama moto

Tashbihi hii inalinganisha kuonesha kwa hasira ya Mungu na moto unaoangamiza vitu. "utatuangamiza"

Psalms 79:6

Taarifa ya Jumla:

Misemo hii miwili yote ina maana za kufanana na inaunganishwa kwa ajili ya kuweka mkazo.

Mwaga gadhabu yako kwa mataifa

Asafu anazungumzia gadhabu ya Mungu kana kwamba ilikuwa ni kimiminiko. "Kwa kuwa una hasira, adhibu mataifa"

haliiti jina lako

Neno "jina" ni njia nyingine ya kusema nguvu na mamlaka ya mtu. "sio wako" au "hawakuombi wewe kuwasaidia"

wamemmeza Yakobo

Neno "Yakobo" ni njia nyingine ya kusema uzao wako, watu wa Israeli. "wamewaangamiza kabisa watu wa Israeli"

Psalms 79:8

Usishikilie dhambi za baba zetu dhidi yetu

"Usiendelee kukumbuka dhambi za baba zetu na kutuadhibu kwa sababu yao" au "Tusamehe kwa dhambi za baba zetu"

tuko chini sana

"tumedhoofika sana"

Mungu wa wokovu wetu

"Mungu anayetuokoa"

kwa ajili ya utukufu wa jina lako

Neno "jina" ni njia nyingine ya kusema sifa yake, kwa kile ambacho watu wanachojua kumhusu. "ili watu wajue kuhusu utukufu wako"

kwa ajili ya jina lako

Jina la Mungu hapa linamwakilisha yeye na heshima anayostahili. "ili watu wakuheshimu" au "kwa ajili yako mwenyewe"

Psalms 79:10

Kwa nini mataifa yasema, "Yuko wapi Mungu wao?"

"Mataifa hayapaswi kusema, 'Yuko wapi Mungu wao?'"

Yuko wapi Mungu wao?

"Mungu wao hawezi kufanya chochote!"

Na damu ya watumishi wako iliyomwaga ilipizwe kisasi juu ya mataifa mbele ya macho yetu

Kumwaga damu ni njia nyingine ya kusema kuua watu wasio na hatia. "Walipize kisasi watumishi wako wasio na hatia ambao mataifa waliwaua ambapo tunaweza kukuona unapofanya hivyo."

mbele ya macho yetu

"machoni petu" au "wakati tupo"

Na kuguma kwa wafungwa kufike mbele yako

Asafu anazungumzia sauti ambayo wafungwa walitoa katika maumivu na huzuni kana kwamba alikuwa ni mtu aliyejitokeza mbele ya mfalme. "Sikiliza kwa usikivu kuguma kwa wafungwa na wasaidie"

wana wa mauti

"wale walio hukumiwa kufa"

Psalms 79:12

Lipa ... matusi yao ... Bwana

Asafu anazungumzia matendo ya uovu ambayo nchi jirani zilifanya dhidi ya Israeli kama "matusi" na kana kwamba ni vitu halisia. Anamwomba Mungu kuhesabu matendo hayo, na kwa kila moja ambayo mataifa jirani yalitenda, anamwomba Mungu kumfanya mtu awafanyie matendo ya uovu saba mataifa jirani.

Lipa

"Warudishie"

mapajani mwao

katika magoti yao na mapaja wakati wanakaa chini. Hii nisitiari ya "moja kwa moja na binafsi."

sisi watu wako na kondoo wa malisho tutakupa shukrani

Neno "kondoo" ni sitiari ya watu wasio jiweza ambao mchungaji anawalinda na kuwaongoza. sisi ambao ni watu wako, ambao unatulinda na kutuongoza, tutakushukuru"

kusema sifa zako kwa vizazi vyote

"hakikisha vizazi vyote vinakuja kufahamu mambo yote mema uliyotenda"

sifa zako

Hii ni njia nyingine ya kusema "mambo mazuri ambayo watu watakusifia"

Psalms 80

Psalms 80:1

Taarifa ya Jumla

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

weka katika Shoshannimu

Hii inaweza kuwa inamaanisha mtindo wa muziki.

Zaburi ya Asafu

"Hii nizaburi ambayo Asafu aliandika."

Mchungaji wa Israeli

Asafu anamzungumzia Mungu kama yule anayeiongoza na kuilinda Israeli.

wewe uliyemwongoza Yusufu kama kundi

"wewe unayewaongoza uzao wa Yusufu kana kwamba ni kundi la kondoo"

Yusufu

Hapa Yusufu inamaanisha taifa la Israeli.

wewe uketiye juu ya makerubi

Mfuniko wa sanduku la agano hekaluni, ishara ya kiti cha enzi ambapo Mungu aliitawala Israeli, ilikuwa imeunganishwa na makerubi ya dhahbu, moja kila upande, zikitazamana.

ung'ae kwetu

Asafu anamzungumzia Mungu kana kwamba ni jua, linalotoa mwanga, sitiari ya unyofu. "tupe mwanga" au "tuoneshe njia sahihi ya kuishi"

tikisa nguvu yako

Msemo "tikisa" inamaanisha "weka katika matendo"

fanya uso wako ung'ae kwetu

Mwandishi anamzungumzia Yahwe kuwatendea kwa fadhila kana kwamba uso wa Yahwe uling'aa mwanga kwao.

na tutaokoka

"na tafadhali tuokoe" au "ili utuokoe"

Psalms 80:4

watu wako

Israeli

Umewalishana mkate wa machozi na kuwapa machozi kunywa kwa wingi

Maneno "mkate wa machozi" na "machozi kunywa" ni sitiari ya huzuni endelevu. "Umehakikisha kuwa wana huzuni sana muda wote"

Psalms 80:7

Taarifa ya Jumla:

Asafu anazungumza kwa niaba ya Israeli. Anaanza katika mstari wa 8 kuzungumzia jinsi Mungu alivyowaweka Israeli katika nchi yao kana kwamba Mungu alikuwa ni mtu anayesafisha ardhi ili kupanda mzabibu.

fanya uso wake ung'ae kwetu

Mwandishi anamzungumzia Yahwe kuwatendea kwa fadhila kana kwamba uso wa yahwe alimulika mwanga juu yao. "tenda kwa fadhila kwetu"

tutaokoa

"utatuokoa"

Unileta mzabibu kutoka Misri

Asafu anafananisha taifa la Israeli na mzabibu uliowekwatayari kwa kupandwa. "Ulituleta, kama mzabibu, kutoka Misri"

uliyaondoa mataifa na ukaupanda tena

Mwandishi wa zaburi anawazungumzia watu wake kana kwamba ni mmea ambao Yahwe alikuwa akiupanda tena. "Uliyaondoa mataifa kutoka katika nchi yao na kutupa sisi mzabibu, nakutupanda huko.

Psalms 80:9

Taarifa ya Jumla:

Asafu anazungumza kwa niaba ya Israeli. Anaanza katika mstari wa 8 kuzungumzia jinsi Mungu alivyowaweka Israeli katika nchi yao kana kwamba Mungu alikuwa ni mtu anayesafisha ardhi ili kupanda mzabibu.

Ulisafisha nchi kwa ajili yake

"Ulisafisha nchi kwa ajili ya mzabibu"

ikasika mzizi

""mzabibu ulikamata mzizi" au "mzabibu ulianza kuota"

kuijaza nchi

"matawi yake yakafunika nchi"

Milima ilifunikw kwa kivuli chake, seda za Mungu kwa matawi yake

"kivuli chake kilifunika milima, matawi yake seda za Mungu"

seda za Mungu kwa matawi yake

"na seda za Mungu zilifunikwa kwa matawi yake" "namatawi yake yalifunika seda za Mungu"

seda za Mungu

Maana zinazowezekana ni 1) "miti ya seda mirefu zaidi," miti ya seda iliyoota kwenye "milima" katika nchi ya Lebanoni kaskazini mwa Israeli, au 2) "Miti ya seda ya Mungu."

bahari

bahari ya Mediteranea magharibi mwa Israeli

vichipukizi

sehemu za mimea ambazo zinaanza kutokeza kutoka ardhini

Psalms 80:12

Taarifa ya Jumla:

Asafu anazungumza kwa niaba ya Israeli. Anaanza katika mstari wa 8 kuzungumzia jinsi Mungu alivyowaweka Israeli katika nchi yao kana kwamba Mungu alikuwa ni mtu anayesafisha ardhi ili kupanda mzabibu.

kuta zake

kuta za mawe, sio za mbao

nguruwe wa msituni

nguruwe pori wanaharibu bustani na mashamba na kuvamia watu.

msitu

ardhi ambapo kuna miti mingi

wanyama

hawa ni wanyama pori wa aina yoyote

shambani

ardhi ambapo kuna mimea mingi lakini hakuna miti

Psalms 80:14

Taarifa ya Jumla:

Asafu anazungumza kwa niaba ya Israeli. Anaanza katika mstari wa 8 kuzungumzia jinsi Mungu alivyowaweka Israeli katika nchi yao kana kwamba Mungu alikuwa ni mtu anayesafisha ardhi ili kupanda mzabibu.

Geuka

"Geuka kwetu" au "Njoo utusaidie tena"

na ugundue

"na uangalie"

mzabibu huu

Mwandishi anaendelea kufananisha taifa la Israeli na mzabibu.

Huu ni mzizi ambao mono wako wa kuume ulipanda

Mkono wa kuume unawakilisha uwezo na nguvu ya Yahwe. "Huu ndio mzizi ambao wewe, Yahwe, ulipanda"

kichipukizi

sehemu za mimea ambazo zinaanza kutokeza kutoka ardhini

chini; wanaangamia kwa sababu ya lawama yako

Maana zinazowezekana ni 1) chini; watu wako wanaangamia kwa sababu ya lawama yako." au 2) "chini. Na adui zako waangamie kwa sababu ya lawama yako!"

Psalms 80:17

mkono wako

Hii inamaanisha uwezo na nguvu ya Yahwe.

mtu wa mkono wako wa kuume

taifa la Israeli, ambalo Yahwe amelichagua kama watu wake

mkono wako wa kuume

Mtu katika Israeli alipotaka kumpa heshima mtu mwingine, alimweka mtu mwingine kusimama katika upande wake wa kuume, karibu na mkono wake wa kuume.

hatutakugeuka

"hatutaacha kukuabudu na kukutii" au "daima tutakuabudu na kukutii wewe"

Psalms 80:19

ung'ae kwetu

Mwandishi anamzungumzia Yahwe kuwatendea kwa fadhila kana kwamba uso wa Yahwe uling'aa mwanga kwao. "tenda kwa fadhila kwetu"

tutaokoka

"utatuokoa"

Psalms 81

Psalms 81:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Taarifa ya Jumla:

Zaburi ya Asafu.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

weka katika Gitithi

Hii inaweza kumaanisha mtindo wa muziki.

Zaburi ya Asafu

"Hii ni zaburi ambayo Asafu aliandika"

Mungu nguvu yetu

"Mungu anayesababisha tuwe na nguvu"

Mungu wa Yakobo

Hapa "Yakobo" inawakilisha uzao wake wote. "Mungu wa israeli, taifa la uzao wa Yakobo"

pigeni tari, kinubi kizuri

Hivi ni vyombo vya muziki.

tari

chombo cha muziki chenye kichwa kama ngoma kinachoweza kugongwa na kina vipande vya chuma vimezunguka pembeni vinavyotoa sauti chombo kinapotikiswa.

mwandamo wa mwezi

Huu ni mwanzo wa mwezi.

siku ya mbalamwezi

Hapa ni katikati ya mwezi.

sikukuu zetu zinapoanza

"na katika siku ambapo sikukuu zetu zinapoanza"

Psalms 81:4

Kwa kuwa

Hapa kinachozungumziwa ni sikukuu.

amri iliyotolewa na Mungu wa Yakobo

"Mungu wa Yakobo aliamrisha" au "Mungu wa yakobo aliamuru"

Mungu wa Yakobo

Hapa "Yakobo" inawakilishwa uzao wake wote. "Mungu wa Israeli, taifa la uzao wa Yakobo"

aliitoa kama kanuni

"aliitoa kama sheria"

katika Yusufu

Hapa "Yusufu" inawakilisha Waisraeli. "kwa Waisraeli"

alipoaende dhidi ya nchi ya Misri

Hii inamaanisha matukio ya kihistoria katika Misri wakati watu wa Israeli walipokuwa watumwa na Mungu akawaokoa.

nchi ya Misri

Hapa "nchi" inawakilisha watu. "watu wa Misri"

Psalms 81:6

Taarifa ya Jumla:

Hapa Mungu anaanza kuzungumza.

Nilitoa mzigo kutoka mabegani mwake

Hapa "mzigo kutoka mabegani mwake" inawakilisha kazi za kulazimishwa ambazo Waisraeli iliwalazimu kufanya kama watumwa Misri.

mikono yake iliwekwa huru na kushikilia kikapu

Hapa "kushikilia kikapu" inawakilisha kazi za kulazimishwa ambazo Waisraeli iliwalazimu kufanya kama watumwa Misri.

katika dhiki yako

"katika mateso yako makuu"

Nilikujibu kutoka katika wingu la giza la radi

Mungu alipokuja kwa Waisraeli, alificha ukamili wa uwepo wake na utukufu katika wingu lenye giza na la kutisha.

Nilikujaribu katika maji ya Meriba

Mungu aliwajaribu wana wa Israeli kuona kama watamtumaini kuwapa maji katika jangwa la Meriba.

Psalms 81:8

Taarifa ya jumla:

Yahwe unawakumbusha watu alichosema wakati wako jangwani.

kwa kuwa nitawaonya

"kwa sababu ninakupa onyo"

Israeli

Hapa "Israeli" inawakilisha watu wa Israeli. "Waisraeli" au "watu wa Israeli"

kama tu utanisikiliza!

"jinsi ninavyotamani kuwa mnisikilize" au "lakani inabidi muanze kunisikiliza!"

Fungua mdomo wako wazi, na nitaujaza

Mungu kujali mahitaji ya watu inazungumziwa kana kwamba alikuwa ni ndege anawalisha makinda yake.

Psalms 81:11

Taarifa ya Jumla:

Sasa Yahwe anaeleza nini kilitokea baada ya kuwaonya watu.

maneno yangu

Hapa "maneno" yanawakilisha kile ambacho Mungu alisema. "kwa kile nilichosema" au "kwangu"

Kwa hiyo nikawapa kwa njia yao wenyewe ya usumbufu

Mungu kuwaruhusu watu kubaki wasumbufu inazungumziwa kana kwamba Mungu alikuwa akiwapa kwa adui kumwacha adui awadhuru. "Kwa hiyo, ninawaacha wawe wasumbufu"

Psalms 81:13

O, kama watu wangu watembee katika njia zangu

Mungu kutaka watu kumtii inazungumziwa kana kwamba alitaka watu kutembea katika njia yake au mabarabara. "natamani kuwa watii sheria zangu"

geuza mkono wako dhidi

Hapa "mkono" inawakilisha uwezo wa yahwe. "nitawaangamiza" au "Nitawaangamiza"

Psalms 81:15

wanaomchukia Yahwe ... mbele zake

Yahwe anajizungumzia mwenyewe katika hali ya mtu wa tatu. ""wanaonichukia ... mbele yangu"

wajikunyate kwa hofu

"inama chini kwa hofu" au "anguka chini kwa hofu"

Na waaibishwe milele

"Nitawaaibisha milele" au "Nitawaadhibu milele"

Nitawalisha israeli kwa ngano safi

Mungu kusababisha ngano bora zaidi kuota Israeli inazungumziwa kana kwamba angewalisha watu ngano kiuhalisia. "Nitawaruhusu Waisraeli kula ngano bora zaidi"

Nitawalisha Israeli ... nitakuridhisha

Hapa pote wanaozungumziwa ni watu wa Israeli.

asali kutoka kwenye mwamba

Hii inamaanisha asali ya porini. Nyuki hujenga mizinga katika mashimo kwenye miamba na kutengeneza asali humo.

Psalms 82

Psalms 82:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Asafu

"Hii ni zaburi ambayo Asafu aliandika"

mkusanyiko mtakatifu

"baraza la mbinguni" au "mkutano wa mbinguni"

anapitisha hukumu

"anatoa hukumu." Nomino dhahania "hukumu" inaweza kuelezwa kama kitenzi. "anahukumu"

miungu

Maana zinazowezekana ni 1) hivi ni viumbe vingine vya kiroho vinavyoishi mbinguni. "viumbe vitakatifu" au "mahakimu wa mbinguni" au 2) hawa ni mahakimu binadamu ambao Mungu amewachagua. Vyovyote vile, haimaanishi ni miungu kama Yahwe alivyo Mungu. Inamaanisha Mungu amewapa uwezo mkubwa na mamlaka. "watawala"

Hadi lini utahukumu bila haki na kuonesha upendeleo kwa waovu?

Yahwe anatumia swali kukemea miungu kwa kutowahukumu watu kwa haki.

Sela

Hili linaweza kuwa neno la kimuziki linalowaongoza watu jinsi ya kuimba au kujecheza vyombo hapa. Tafsiri zingine huandika neno hili la Kiebrania, na zingine haziliweki.

Psalms 82:3

maskini na wasio na baba

Hapa "maskini" na "wasio na baba" vivumishi vidogo. Vinaweza kuelezwa kama vivumishi. "wale walio maskini na walio yatima"

tunza haki za

"fanya iliyo haki kwa"

walioteswa na fukara

Hapa "walioteswa" na "fukara" ni vivumishi vidogo. Vinaweza kuelezwa kama vivumishi. "wale wanaoteseka na wale wasiokuwa na kitu"

maskini na wahitaji ... waovu

Hivi ni vivumishi vidogo. Vinaweza kuelezwa kama vivumishi. "wale walio maskini na wale walio wahitaji ... wale walio waovu"

watoe katika mkono wa waovu

Hapa neno "mkono" inawakilisha nguvu au uwezo. "uwadhibiti waovu kuwadhuru"

Psalms 82:5

Hawaelewi

Maana zinazowezekana ni 1) wasioelewa ni miungu au 2) wasioelewa ni watu waovu.

wanazurura gizani

Kufanya kilicho kiovu kinazungumziwa kana kwamba walikuwa wakitembea sehemu yenye giza sana.

misingi yote ya duniani inaanguka

Miungu kuharibu mpangilio wa uadilifu ambao Yahwe aliweka inazungumziwa kana kwamba miungu ilikuwa inatikisa dunia na kuifanya ibomoke.

inaanguka

"kubomoka"

Psalms 82:6

Nyie ni miungu, na nyie wote ni wana wa Aliye juu

Hapa "miungu" inamaanisha kundi sawa na la Zaburi 82:1. Kama hii inamaanisha viumbe wa kiroho au binadamu, sio miungu kama Yahwe alivyo Mungu, na sio wana wake kihalisi. Kwa kuwaita "miungu" na "wana wa Aliye juu," Yahwe anakiri kuwa amewapa uwezo mkuu na mamlaka.

wana wa Aliye juu

Yahwe anajizungumzia mwenyewe kama "Aliye juu."

Hata hivyo

"Ingawa"

na kuanguka

Hii ni njia ya kuzungumzia mtu anayekufa.

Psalms 82:8

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anazungumza tena.

hukumu ulimwengu

Hapa "ulimwengu" unawakilisha watu. "hukumu watu wa ulimwengu"

kwa kuwa una urithi katika mataifa yote

"kwa kuwa mataifa yote ni urithi wako." Yahwe kuwachukua watu wote kama wake na kuwatawala inazungumziwa kana kwamba mataifa ni mali aliyorithi. "kwa kuwa unatawala juu ya watu wote wa kila taifa"

maataifa yote

Hapa "mataifa" inawakilisha watu wa mataifa.

Psalms 83

Psalms 83:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Wimbo. Zaburi ya Asafu

"Hii ni zaburi ambayo Asafu aliandika"

na kubaki bila kusogea

"na kutokufanya kitu kutusaidia"

Tazama, adui zako wanafanya ghasia

Hapa "kufanya ghasia" inamaanisha kufanya fujo au kukaidi. "Tazama, adui zako wanakaidi dhidi yako"

wale wanokuchukia wameinua vichwa vyao

Msemo "wameinua vichwa vyao" ni njia ya kusema kuwa wamekaidi dhidi ya Mungu. "wale wanaokuchukia wanakukaidi"

Psalms 83:3

uliowalinda

"wale unaowalinda" Hii inamaanisha Waisraeli.

jina la Israeli halitakumbukwa tena

Hapa "jina" linawakilisha sifa au kumbukumbu ya mtu. "hakuna mtu atakye kumbumbuka Waisraeli walikuwepo"

Wamepanga hila kwa pamoja na mkakati mmoja

"Adui zako wamekubali pamoja kwa mpango mmoja"

dhidi yako wamefanya mwungano

"wameungana pamoja dhidi yako"

Psalms 83:6

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaendelea kuorodhesha makundi ya watu yanayotaka kuangamiza Israeli.

mahema ya Edomu

Hii inamaanisha watu wa Edomu walioishi katika mahema.

Wahagari

Hili ni jina la kundi la watu walioishi upande wa mashariki wa mto Yordani.

Gebali, Amoni, Amaleki ... FIlisti

Majina haya yote yanawakilisha watu wa kila eneo au kabila. "watu wa Gebali, Waamoni, Waamaleki ... Wafilisti"

Gebali

Hili jina la eneo kusini mwa bahari ya Chumvi.

Psalms 83:8

Ashuri

Hii inawakilishwa watu wa ashuri. "watu wa Ashuri"

uzao wa Lutu

Hii inamaanisha watu wa mataifa ya Moabu na Amoni.

Sela

Hili linaweza kuwa neno la kimuziki linalowaongoza watu jinsi ya kuimba au kujecheza vyombo hapa. Tafsiri zingine huandika neno hili la Kiebrania, na zingine haziliweki.

Psalms 83:9

Fanya kwao ...kwa ajili ya dunia

Mwandishi anamwomba Mungu kuwashinda adui wa Israeli kama alivyofanya kipindi cha nyuma.

ulivyofanya kwa Midiani

Hapa "Midiani" inawakilishwa watu wa Midiani. "ulivyofanya kwa Wamidiani"

Sisera ... Yabini

Haya ni najina ya wanaume. Yabini alikuwa mfalme wa Hazori. Sisera alikuwa kamanda wa jeshi la Yabini.

mto Kishoni

Hili ni jina la mto kaskazini mwa israeli

Endori

Hili ni jina la mji kaskazini mwa Israeli,

wakawa kama mbolea kwa ajili ya dunia

Hii inamaanisha miili ya Sisera na Yabini haikuzikwa lakini iliachwa kuoza.

Psalms 83:11

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anamwomba Mungu kuwashinda adui wa Israeli kama alivyofanya kipindi cha nyuma.

Orebu ... Zeebu ... Zeba ... Zalmuna

Haya yote ni majina ya wafalme.

Wakasema

Hapa "Wakasema" inamaanisha Orebu, Zeebu, Zeba na Zalmuna.

malisho ya Mungu

Mwandishi anazungumzia nchi ya Israeli kana kwamba ni nchi kwa ajili ya kondoo kula na Mungu alikuwa mchungaji wao aliyekuwa akiwachunga.

Psalms 83:13

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anatumia tashbihi kuelezea uharibifu kamili wa Mungu kwa adui wa Israeli.

wafanya kuwa kama mavumbi yanayozunguka, kama makapi mbele ya upepo

Kauli zote mbili zinazungumzia Mungu kuangamiza adui zake kana kwamba alikuwa upepo mkali unaowapuliza kwa urahisi.

kama moto unaochoma msitu, na moto unaoweka milima katika moto

Kauli zote mbili zinazungumzia adhabu ya Mungu kana kwamba ni moto, na adui wa Mungu ni vitu vinavyoungua katika moto.

Wafukuze kwa upepo wako wenye nguvu, na watishe kwa dhoruba yako

Kauli zote mbili zinamwomba Mungu kuangamiza adui kwa dhoruba.

Psalms 83:16

Jaza nyuso zao na aibu

Hapa "nyuso"zinawakilishwa mtu mzima. "Wafanye waaibike sana"

watafute jina lako

Hapa "jina" linawakilisha uwezo wa Mungu. Adui wa Mungu kukiri kuwa Mungu ana uwezo inazungumziwa kana kwamba wanatafuta kumpata yahwe. "wakubali kuwa una uwezo"

watafute jina lako

Maana zinazowezekana ni 1) adui wa Mungu wanakiri kuwa Mungu ana uwezo au 2) adui wa mungu wanamwomba Mungu msaada au 3) adui wa Mungu wanaanza kumwabudu na kumtii.

Na waaibishwe na kuogofywa milele

"Wafanye waaibike na kuogopa milele"

waangamie kwa aibu

"na wafe wakiwa wameaibika"

Psalms 83:18

Kisha watajua

"Wafanye wajue"

ndiye Uliye juu, juu ya dunia yote

Mungu kutawala juu kila kitu duniani inazungumziwa kana kwamba ameinuliwa juu zaidi ya vingine vyote. "ndiye mkuu, na unatawala vitu vyote duniani"

Psalms 84

Psalms 84:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

weka katika Gitithi

Hii inaweza kuwa inamaanisha mtindo wa muziki.

Zaburi ya wana wa Kora

"Hii ni zaburi ambayo wana wa Kora waliandika"

Panapendeza kiasi gani

"Ni pazuri kiasi gani"

na shauku na nyua za Yahwe

"Ninatamani sana kuwa katika nyua za Yahwe"

nyua za Yahwe

Hapa "nyua" inawakilisha hekalu.

hamu yangu kwa kwa hizo imanichosha

"hamu yangu imenichosha" au "nimechoka kwa sababu ninaitaka sana"

Moyo wanguna kila kitu ndani yangu kinamwita

Hapa "moyo" unawakilisha mtu mzima. "Niita kwa kila kitu ndani yangu"

Mungu aliye hai

Hii inamaanisha kuwa Mungu yu hai na pia ana uwezo wa kusababisha vitu vingine kuishi.

Psalms 84:3

shorewanda ... mbayuwayu

Hawa ni aina ya ndege.

amepata nyumba

"amejipatia makazi" au "ametengeneza makazi"

mbayuwayu kioto

"mbayuwayu amepata kioto" au "mbayuwayu ametengeneza kioto"

ambapo anaweza kuweka makinda yake

"ambapo anaweza kutaga mayai na kutunza makinda yake"

wale wanaoishi nyumbani kwako

Maana zinazowezekana ni 1) "wale' inamaanisha makuhani ambao hutumika muda wote hekaluni au 2) "wale" inamaanisha watu kwa ujumla ambao hua wanakuja kuabudu hekaluni.

kwa uendelevu

"tena na tena"

Psalms 84:5

Amebarikiwe mtu

Hapa "mtu" inamaanisha watu kwa ujumla.

ambaye nguvu yake iko katika wewe

Mungu anazungumziwa kana kwamba nguvu kweli ilipatikana ndani yake. "ambaye unamtia nguvu"

ambaye moyoni mwake ni njia za kwenda Sayuni

Msemo huu unahusu hamu ya kweli kutoka moyoni. "Wanaopenda kwenda juu Sayuni" au "Wanaotaka kwa dhati kwenda juu Sayuni"

njia

"barabara kuu"

za kwenda Sayuni

Hekalu lilikuwa Yerusalemu juu ya kilima kirefu zaidi, kiitwacho mlima Sayuni.

mabonde ya Machozi

Hii inamaanisha sehemu iliyokauka. Biblia zingine zina "bonde la Baka." neno "Baka" linamaanisha kulia."

Mvua za mapema

Hii inamaanisha mvua inayodondoka katika majira ya kupukutika kwa majani kabla ya majira ya baridi. Hiki ni kipindi cha miezi ya Oktoba na Novemba katika kalenda za magharibi.

baraka

"mabwawa ya maji"

Psalms 84:7

Huenda kutoka nguvu hadi nguvu

Hii ni njia ya kusema wanapata nguvu.

Huenda

Hapa wanaoenda inamaanisha wale wanaotamani kwenda hekaluni kumwabudu Mungu.

Sela

Hili linaweza kuwa neno la kimuziki linalowaongoza watu jinsi ya kuimba au kujecheza vyombo hapa. Tafsiri zingine huandika neno hili la Kiebrania, na zingine haziliweki.

Mungu, angalia ngao yetu

Mfalme anayewalinda watu wake anazungumziwa kana kwamba ni ngao. "Mungu, mwangalie mfalme wetu"

Kwa kuwa siku moja katika nyua zako ni bora kuliko siku elfu pengine

"Ni bora niwe katika nyua zako kwa siku moja badala ya kuwa sehemu nyingine kwa siku elfu moja"

elfu

"1,000"

niwe bawabu

"niwe mlinzi mlangoni" au "nisimame mlangoni"

waovu

"watu waovu" au "wale ambao ni waovu"

Psalms 84:11

Kwa kuwa Yahwe Mungu ni jua letu na ngao

Yahwe anayewaongoza na kuwalinda watu wake anazungumziwa kana kwamba alikuwa jua na ngao. "Kwa kuwa Yahwe hutuongoza kama mwanga wa jua, na hutulinda kama ngao"

Yahwe atatoa neema na utukufu

"Yahwe atakuwa na huruma kwetu na kutupa heshima"

wanaotembea katika uadilifu

Jinsi mtu anavyoenenda maisha yake inazungumziwa kana kwamba mtu huyo alikuwa akitembea. "wanaoishi kwa uadilifu" au "walio wa kweli"

amebarikiwa mtu

Hapa "mtu" inamaanisha mtu kwa ujumla. "wamebarikiwa wale"

Psalms 85

Psalms 85:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Zaburi ya wana wa Kora

"Hii ni zaburi ambayo wana wa Kora waliandika."

umeonesha fadhila kwa nchi yako

Hapa "nchi" inawakilisha taifa na watu wa Israeli.

ustawi

Hii inamaanisha mtu kuwa na furaha, mwenye afya na mafanikio.

wa Yakobo

Hapa "Yakobo" inawakilisha uzao wa Yakobo, Waisraeli.

umefunika dhambi zao zote

Hapa dhambi iliyosamehewa inazungumziwa kana kwamba imefunikwa ili isionekane. "umesahau kwa makusudi dhambi zao"

dhambi zao

Mwandishi alijifikiria kama kuwa miongoni mwa watu wa Mungu. "dhambi zetu"

Sela

Hili linaweza kuwa neno la kimuziki linalowaongoza watu jinsi ya kuimba au kujecheza vyombo hapa. Tafsiri zingine huandika neno hili la Kiebrania, na zingine haziliweki.

Psalms 85:3

Umeondoa gadhabu yako yote

Mungu kutowaadhibu tena Waisraeli inazungumziwa kana kwamba gadhabu ni kitu ambacho Yahwe anaweza kuondoa kutoka kwa Waisraeli.

umegeuka kutoka katika hasira yako ya moto

Mungu kutokuwa na hasira tena na Waisraeli inazungumziwa kana kwamba hasira ni moto kutoka kwa Mungu ambao Mungu ameuguza.

Mungu wa wokovu wetu

"Mungu anayetuokoa"

achia chuki uliyonayo kwetu

Kumwomba Mungukuacha kuwa na hasira na Waisraeli inazungumziwa kana kwamba chuki ni kitu ambacho mwandishi anataka Mungu aachie.

Je! Utakuwa na hasira na sisi milele? Utabaki na hasira katika vizazi vyote?

Mwandishi anatumia maswali haya kusisitiza kwamba anamwomba Mungu kuacha kuwa na hasira nao. "Tafadhali usibaka na hasira na sisi milele."

Psalms 85:6

Je! Hautahuisha tena?

Mwandishi anatumia swali hili kusisitiza kwamba anamwomba Mungu kuwafanya watu wa Israeli wafanikiwe na wawe na furaha tena. "Tafadhali tufanye kuwa na mafanikio tena"

Tuoneshe uaminifu wako wa agano

"Kuwa mwaminifu kwa sababu ya agano lako na sisi"

tupe wokovu wako

"tupe wokovu wako kwa kutuokoa"

Psalms 85:8

atafanya amani na watu wake

"atakuwa na mahusiano ya amani na watu wake" au "ataleta amani kwa watu wake"

Bali wasirudie tena njia zao za upumbavu

Mtu anayebadili tabia yake anazungumziwa kana kwamba alikuwa akigeukia kimwili upande mwingine. "Bali hawatakiwa kuanza kufanya mambo ya upambavu tena"

Hakika wokovu wake uko karibu na wale

Mungu kuwa tayari kumwokoa mtu inazungumziwa kana kwamba wokovu ni kitu ambacho Mungu ameweka karibu na mtu. "Hakika Mungu yuko tayari kuwaokoa wale"

kisha utukufu utabaki katika nchi yetu

Hapa "utukufu" unawakilisha uwepo wa Mungu. "kisha uwepo wake wa utukufu utabaki katika nchi yetu"

Psalms 85:10

Uaminifu wa agano na uaminifu umekutana pamoja

Maana zinazowezekana ni 1) Mungu atakuwa mwaminifu kwa sababu ya agano lake na atafanya alichoahidi au 2) Mungu atakuwa mwaminifu kwa sababu ya agano lake na watu wataitikia kwa kuwa waaminifu kwake. Vyovyote vile uaminifu unazungumziwa kana kwamba ni mtu anayeweza kukutana na mwenzake.

umekutana pamoja ... zimepigana busu

Inawezekana kuwa mwandishi anazungumzia wakati wa mbele ambapo Mungu atawasababisha watu wake kufanikiwa tena. zitakutana pamoja ... zitapigana busu"

haki na amani zimepigana busu

Maana zinaziwezekana ni 1) watu watafanya kilicho sawa na mungu atawasababisha watu kuishi kwa amani au 2) Mungu atafanya kilicho sawa na kuwasababisha watu kuishi katika amani. Vyovyote vile, haki na amani zinazungumziwa kana kwamba ni watu wanajipiga busu.

zimepigana busu

Hii ni njia ya kawaida ya marafiki kusalimiana.

Uaminifu unachomoza kutoka kwenye ardhi

Watu wa duniani kuwa waaminifu kwa Mungu inazungumziwa kana kwamba uaminifu ni mmea unaoota ardhini. "Hapa duniani, tutakuwa waaminifu kwa Mungu"

haki inaangalia chini kutoka angani

Mwandishi anaelezea haki kama mtu anatazama chin kama Mungu afanyavyo. "Mungu atatuangalia kwa fadhila na kutupa ushinid"

Psalms 85:12

Haki itamtangulia na kutengeneza njia kwa ajili ya hatua zake

Mungu kufanya kilicho sawa kila sehemu aendayo inazungumziwa kana kwamba haki ni mtu ambaye humtangulia Mungu na kuandaa njia ya Mungu kupitia.

hatua zake

Hapa "hatua" inawakilisha ambapo Mungu anapita.

Psalms 86

Psalms 86:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

maskini na niliye kandamizwa

"mnyonge na mhitaji"

mwokoe mtumishi wako

Daudi anajizungumzia kama "mtumishi wako," yaani, mtumishi wa Mungu. "niokoe mimi, mtumishi wako"

Psalms 86:3

siku nzima

Hii ni kukuza kwa neno. Daudi halii siku nzima kwa uhalisia. Hii inasisitiza kuwa huwa analia kwa uendelevu. "kwa uendelevu"

Mfanye mtumishi wako kuwa na furaha

Daudi anajizungumzia kama "mtumishi wako," yaani, mtumishi wa Mungu. "Nifanye mimi, mtumishi wako" au "Nifanye"

Psalms 86:5

Katika siku ya taabu yangu

Hapa "siku" inawakilisha muda mrefu zaidi. "Wakati wa kipindi changu cha taabu"

ninakuita wewe

"nina omba kwako"

Psalms 86:8

kati ya miungu

Mwandishi hakiri kuwa miungu hii mingine ipo. Anamaanisha miungu ya uongo ambayo watu wa mataifa mengine huabudu.

Mataifa yote

Hapa "mataifa" inawakilisha watu. "Watu kutoka mataifa yote"

Watatukuza jina lako

Hapa "jina" linamwakilisha mtu mzima. "Watakutukuza"

Psalms 86:10

mambo ya ajabu

"vitu vizuri sana vinavyo tushangaza"

wewe pekee ni Mungu

"wewe ndiye Mungu pekee"

Nifundishe njia zako, Yahwe. Kisha nitatembea katika kweli yako

Mtu anayetii kile ambacho Mungu anataka anazungumziwa kana kwamba anatembea katika njia au barabara la Mungu. "Nifundishe ukweli wako, Yahwe. Kisha nitatii unachosema"

Unganisha moyo wako kukucha wewe

Hapa "moyo" unawakilisha mawazo, hisia na nia ya mtu. Kumwomba Mungu kumsababisha mtu kumtii kikamilifu inazungumziwa kana kwamba moyo wa mtu ulikuwa katika vipande vingi na kwamba Mungu anaviunganisha pamoja. "Nisababishe nikuheshimu kwa moyo wangu wote" au "Nisababishe nikuheshimu kwa dhati"

nitakusifu kwa moyo wangu wote

Hapa "moyo" unawakilisha mawazo, hisia na nia ya mtu. "Nitakusifu kikamilifu na kwa dhati"

nitalitukuza jina lako

Hapa "jina" linamwakilisha mtu mzima. "nitakutukuza"

Psalms 86:13

Kwa kuwa uaminifu wako wa agano ni mkuu kwangu

"Kwa kuwa wewe ni mwaminifu kwangu kwa sababu ya agano lako"

umeokoa maisha kutoka vilindi vya kuzimu

Hii haimaanishi kuwa Mungu alimfufua baada ya kufa. Inamaanisha kuwa Mungu alimwokoa alipotaka kufa.

wenye kiburi

"watu wenye kiburi"

wameinukadhidi yangu

"wanakuja pamoja kunidhuru"

wanatafuta maisha yangu

Hii ni njia ya kusema wanataka kumuua.

Psalms 86:15

umejaa uaminifu wa agano na uaminifu

Mungu kuwa mwaminifu kila wakati inazungumziwa kana kwamba uaminifu ni kitu ambacho Mungu ana kiasi kikubwa chake.

Geuka kwangu

Kumwomba Mung kumzingatia inazungumziwa kana kwamba alimtaka Mungu amgeukie na kumwangalia.

mpe mtumishi wako nguvu yako

"mwimarishe mtumishi wako" au "mfanye mtumishi wako kuwa imara"

mtumishi wako ... mwana wa mjakazi wako

Mwandishi anajizungumzia mwenyewe katika hali ya mtu wa tatu.

na kuaibishwa

"na wataaibika"

Psalms 87

Psalms 87:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya wana wa Kora; wimbo

"Hii ni zaburi ambayo wana wa Kora waliandika"

malango ya Sayuni

Hapa "malango ya Sayuni" inawakilisha mji mzima wa Yerusalemu. "mji wa Yerusalemu"

mahema yote ya Yakobo

Watu waliishi katika mahema walipokuwa wakizurura jangwani. Hapa mwandishi anatumia "mahema ya Yakobo" kuwakilisha mahali Waisraeli wanapoishi sasa. "sehemu yoyote ya kuishi ya Waisraeli"

Mambo yenye utukufu yanasemwa juu yako, mji wa Mungu

Mwandishi anazungumza na mji wa Yerusalemu kana kwamba ulikuwa unamsikiliza. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Nyie watu katika Yerusalemu, watu wengine wanasema vitu vizuri kuhusu mji wenu"

Sela

Hili linaweza kuwa neno la kimuziki linalowaongoza watu jinsi ya kuimba au kujecheza vyombo hapa. Tafsiri zingine huandika neno hili la Kiebrania, na zingine haziliweki.

Psalms 87:4

Ninamtaja

"Nitawaambia kuhusu." Anyezungumza hapa ni Yahwe.

Rahabu na Babeli

Hapa "Rahabu" ni njia ya kishahiri ya kumaanisha Misri. Zote "Rahabu" na "Babeli" zinawakilisha watu. "watu wa Misri na Babeli"

kwa wafuasi wangu

"kwa wale wanaoniabudu"

Filisti, na Tirohopia, pamoja na Kushi

Majina ya mataifa haya yanawakilisha watu. "watu kutoka Filist na Tiro, pamoja na watu wa Kushi"

Huyu alizaliwa huko

"Huyu" inamaanisha watu kutoka mataifa ambayo mwandisha ameyataja. Ingawa hawakuzaliwa kimwili Sayuni, wale wanaomfuata Mungu ni wakazi wa Yerusalemu kiroho.

Psalms 87:5

Kwa Sayuni itasemwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Watu watasema kuhusu Sayuni"

Kila mmoja wa hawa alizaliwa ndani yake

Watu kutoka mataifa mengine wanaomwabudu Yahwe wanazungumziwa kana kwamba walizaliwa Yerusalemu. "Ni kana kwamba watu hawa wote walizaliwa Yerusalemu"

ndani yake

Ilikuwa kawaida kuelezea miji kama mtu.

Aliye juu mwenyewe

Mwandishi anatumia kiwakilishi cha kujirudia "mwenyewe" kusisitiza kuwa Aliye juu ndiye anafanya hiki.

atamuimarisha

"ataifanya Yerusalemu kuwa imara"

Yahwe anaandika katika kitabu cha sensa cha mataifa

Yahwe kukubali kuwa watu kutoka mataifa mengine ni wake inazungumziwa kana kwamba yeye ni mfalme anayeandika majina ya watu wanaoishi katika mji wake.

Huyu hapa alizaliwa huko

"Huyu" inamaanisha watu kutoka mataifa ambayo mwandishi ametaja. Ingawa hawakuzaliwa kimwili Sayuni, wale wanaomfuata Mungu ni wakazi wa Mji wa Yerusalemu kiroho.

Psalms 87:7

Chemchemi zangu zote ziko ndani yako

Yerusalemu kuwa sehemu ambayo watu hupokea baraka zao zote inazungumziwa kana kwamba Yerusalemu ni chemchemi inayotoa maji kwa watu.

Psalms 88

Psalms 88:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Wimbo, zaburi ya wana wa Kora

"Hii ni zaburi ambayo wana wa Kora waliandika"

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

weka katika mtindo wa Mahalathi Leanothi

Hii inaweza kuwa inamaanisha mtindo wa muziki.

Maschili

Hii inaweza kuwa inamaanisha mtindo wa muziki.

Hemani

Hili ni jina la mwanamume

Mwezrahi

Hili ni jina la kundi la watu. Inaweza kumaanisha mwana au uzao wa Zera.

Mungu wa wokovu wangu

"wewe ndiye unaye niokoa"

mchana na usiku

Mwandishi anatumia maneno haya yenye maana tofauti kumaanisha kuwa analia kwa uendelevu.

Psalms 88:3

Kwa kuwa nimejaa taabu

Mwandishi anajizungumzia kana kwamba ni chombo na taabu ni vitu vinavyojaza hicho chombo. "Kwa kuwa nina taabu sana"

maisha yangu yamefika kuzimu

Hapa "maisha" yanamwakilisha mwandishi na "kuzimi" kunawakilisha mauti. Inawezekana mwandishi anajizungumzia mwenyewe kufa mapema kana kwamba kuzimu ni sehemu na amefika hiyo sehemu. "nimekaribia kufa"

Watu wananifanyia kama wale wanaoenda chini shimoni

Neno "shimo" linamaana moja kama "kuzimu." Msemo "wanaoenda chini kuzimu" inawakilisha kufa. "watu wananifanya kana kwamba tayari nimekufa"

Psalms 88:5

Nimeachwa miongoni mwa wafu

Watu kumfanyia mwandishi kana kwamba tayari amekufa inazungumziwa kana kwamba ni maiti ambayo imeachwa bila kuzikwa. "Nimeachwa peke yangu kana kwamba nimekufa"

mimi ni kama mfu niliyelala kaburini

Mwandishi kuhisi kana kwamba watu na Mungu wamemwacha anajizungumzia kana kwamba alikuwa tayari ni mtu aliyekufa amelala kaburini.

mfu niliyelala

"mtu aliyekufa mabaye amelala" au "watu waliokufa ambao wamelala"

ambao huwajali tena

"watu ambao umeacha kuwajali"

wamekatwa kutoka katika nguvu yako

Mungu kuacha kutumia nguvu yake kuwasaidia wafu inazungumziwa kana kwamba Mungu amemkata au amemtoa kutoka kwenye nguvu yake. "hautumii tena nguvu yako kuwaokoa"

Umeniweka katika sehemu ya chini zaidi ya shimo, katika vina vya china vyenye giza

Mwandishi kuhisi kama Mungu kumwacha anajizungumzia kana kwamba Mungu amemweka katika kaburi kina kirefu zaidi na lenye giza.

Psalms 88:7

Gadhabu yako ni nzito kwangu

Hii inazungumzia jinzi Mungu alivyo na hasira sana na mwandishi kana kwamba gadhabu ya Mungu ni kitu kizito kilicho juu ya maji. "Ninahisi hasira yako kuu" au "Ninahisi jinsi ulivyo na hasira kali na mimi"

njia zako zote zinanikandamiza

Hii inazungumzia Mungu kuwa na hasira sana na mwandishi kana kwamba hasira ya Mungu ni mawimbi makubwa yanayoinuka kutoka baharini na kutua kwa mwandishi.

Sela

Hili linaweza kuwa neno la kimuziki linalowaongoza watu jinsi ya kuimba au kujecheza vyombo hapa. Tafsiri zingine huandika neno hili la Kiebrania, na zingine haziliweki.

Psalms 88:8

wanaonifahamu

"wale wanaonijua"

Umenifanya kitu cha kushangaza kwao

"Umenifanya kitu cha kuchukiza machoni kwao" au "Kwa sababu yako, wanashangaa wanaponiona"

Nimezungukwa

Hali ya kimwili ya mwandishi inayomfanya kuwa chukizo kwa rafiki zake inazungumziwa kana kwamba alikuwa amefungwa katika nafasi yenye mipaka. "Ni kana kwamba nilikuwa gerezani" au "Nimenaswa"

Psalms 88:9

Macho yangu yanachoka kutokana na taabu

Hapa "macho" yanawakilisha uwezo wa mtu kuona. Kwa macho yake kuchoka kutokana na taabu ni njia ya kusema kwamba matatizo yake yanamsababisha kulia sana hadi inakuwa kazi kwake kuona.

Ninanyosha mikono yangu kwako

"Ninainua mikono yangu kwako." Hiki ni kitendo kinachoonesha kuwa anamtegemea Mungu kabisa.

Je! Utafanya maajabu kwa wafu?

Mwandishi anatumia swali kusisitiza kuwa kama Mungu akimwacha afe basi Mungu hataweza tena kufanya mambo ya ajabu kwa ajili yake. "Wewe hufanyi maajabu kwa awatu waliokufa."

Je! Wale waliokufa watafufuka na kukusifu

Mwandishi anatumia swali kusisitiza kuwa kama Mungu akimwacha afe basi hataweza kumsifu Mungu tena. "Unajua kuwa waliokufa hawataweza kusimama na kukusifu"

Psalms 88:11

Je! Uaminifu wako wa agano utatangazwa kaburini, uaminifu wako katika sehemu ya wafu?

Maswali yote yanamaanisha kitu kimoja. Mwandishi anatumia maswali kusisitiza kuwa mtu aliyekufa hawezi kusifu uaminifu wa Mungu. "Hakuna atakaye tangaza uaminifu wako wa agano au uaminifu wako kutoka kaburini"

kaburini ... sehemu ya wafu ... gizani ... sehemu ya usahaulifu

Majina haya yote yanawakilisha mahali ambapo watu huenda baada ya kufa.

uaminifu wako katika sehemu ya wafu?

"Je! Uaminifu wako utatangazwa katika sehemu ya wafu?" au "Wale waliokufa hawatatangaza uaminifu wako."

Je! Matendo yako ya ajabu yatajulikana gizani, au haki yako katika sehemu ya haki?

Maswali yote yanamaanisha kitu kimoja. Mwandishi anatumia maswali kusisitza kuwa wale walio kufa hawawezi kupitiia au kutangaza mambo makuu ambayo Mungu hufanya. "Watu hawazungumzii kuhusu matendo yako ya ajabu na haki katika sehemu ya giza ya watu walio sahaulika."

au haki yako katika sehemu ya haki?

"Je! Haki yako itajulikana katika sehemu ya walio sahaulika?" au "Wale walio katika sehemu ya usahaulifi hawatajua kuhusu mambo ya haki unayofanya."

Psalms 88:13

ombi langu linafika mbele yako

Mwandishi kuomba kwa yahwe inazungumziwa kana kwamba ombi lenyewe linaenda kuzungumza na Yahwe.

Kwa nini unaficha uso wako kwangu?

Hii inazungumzia mwandishi kuhisi kama Mungu amemkataa au kumwacha kana kwamba Mungu alikuwa akificha sura yake au kugeuka kiuhalisia kumwepuka mwandishi.

Psalms 88:15

Matendo yako ya hasira yamepita juu yangu

Hii inamzungumzia Mungu kumwadhibu mwandishi kana kwamba matendo ya Mungu ni wimbi kubwa linaloinuka kutoka baharini na kumwangukia na kumkandamiza mwandishi. "ni kana kwamba matendo yako ya hasira yananikandamiza"

matendo yako ya kutisha yameniangamiza

Hii inazungumzia Mungu kumwadhibu mwandishi kana kwamba Mungu alimwangamiza kabisa mwandishi. "vitu vya kutishi unavyofanya vimeniangamiza" au "vitu vya kustisha unavyofanya kidogo viniangamize"

Psalms 88:17

Yamenizunguka kama maji siku nzima

Mwandishi anafananisha m"matendo ya hasira" ya Mungu na "matendo ya kutisha" na mafuriko ya maji. "Siku nzima wananitisha kuniangamiza kama mafuriko"

Yamenizunguka

Kinachozungumziwa ni "matendo ya hasira" ya Mungu na "matendo ya kutisha" kutoka katika mstari uliopita.

yamenizunguka yote

Mwandishianazungumzia "matendo ya hasira" na "matendo ya kutisha" kana kwamba ni adui waliokuwa wakijaribu kumshika na kumuua. "wamenizunguka kama askari adui"

kila rafiki na anaye nijua

"kila mtu ninayempenda na kumjua"

Anijuae pekee ni giza

Hii inazungumzia giza kana kwamba ni mtu ambaye anaweza kuwa rafiki na mtu mwingine. Mwandishi anasisitiza kuwa anajihisi upweke. "Kila sehemu ninayoenda ni giza"

Psalms 89

Psalms 89:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Maschili

Hii inaweza kumaanisha mtindo wa muziki.

Ethani

Hili ni jina la mwandishi.

Mwezrahi

Hili ni jina la kundi la watu. Inaweza kumaanisha mwana au uzao wa Zera.

matendo ya uaminifu wa agano

"matendo ya uaminifu" au "matendo ya upendo"

Uaminifu wa agano umethibitishwa milele

Mungu kufanya alichoahidi kufanya inazungumziwa kana kwamba uaminifu wake ni jengo ambalo Mungu amejenga na kuimarisha. "Daima utakuwa mwaminifu kwa sababu y agano lako na sisi"

ukweli wako umethibitisha mbinguni

Mungu kufanya alichoahidi kufanya inazungumziwa kana kwamba uaminifu wake ni jengo ambalo Mungu amejenga na kuimarisha.

mbinguni

Maana zinazowezekana ni 1) hii inamaanisha makazi ya Mungu. Hii inamaanisha Mungu hutawala kutoka mbinguni na huwa anafanya kile alichoahidi au 2) hii inamaanisha anga. Hii inamaanisha kuwa wahadi za Mungu hazibadiliki na ni za kudumu kama anga.

Psalms 89:3

Nimefanya agano na niliye mchagua

"Nimempa ahadi Daudi, yule niliye mchagua"

Nimefanya

Yahwe anazungumza katika 89:3-4.

Nitawathibitisha uzao wako milele

Yahwe kuwasababisha uzao wa Daudi daima kuwa wafalme inazungumziwa kana kwamba uzao wa Daudi ni jengo ambalo Yahwe atajenga na kuimarisha.

Nitathibitisha kiti chako cha enzi katika vizazi vyote

Hapa "kiti cha enzi" kinawakilisha uwezo wa kutawala kama mfalme. Mwandishi wa zaburi anazungumzia Mungu kuahidi kuwa mmoja wa uzao wa Daudi atatawala daima kama mfalme kana kwamba Mungu atajenga kiti cha enzi cha Daudi na kukiimarisha. "Nitahakikisha kwamba mmoja wa uzao wako atatawala kama mfalme juu ya kila kizazi cha watu wangu"

Sela

Hili linaweza kuwa neno la kimuziki linalowaongoza watu jinsi ya kuimba au kujecheza vyombo hapa. Tafsiri zingine huandika neno hili la Kiebrania, na zingine haziliweki.

Psalms 89:5

Mbingu zinasifu

Hapa "mbingu" inawakilisha wale walio mbinguni.

zinasifu maajabu yako, Yahwe

"zinakusifu, Yahwe, kwa sababu ya mambo ya ajabu unayotenda"

ukweli wako unasifiwa katika kusanyiko la watakatifu wako

"Mkusanyiko wa watakatifu hukusifu kwa sababu daima huwa unafanya ulichoahidi kufanya"

kusanyiko la watakatifu wako

Hii inamaanisha malaika mbinguni.

Kwa kuwa ni nani angani anaweza kulinganishwa na Yahwe? Nani miongoni mwa wana wa miungu ni kama Yahwe?

Maswali haya yote yana maana moja. Mwandishi anatumia swali hili kusisitiza kuwa hakuna mtu kama Yahwe mbinguni.

wana wa miungu

Hapa "wana" inamaanisha kuwa na sifa za. HIi ni njia ya kumaanisha viumbe vya kiroho vinavyoishi mbinguni. "malaika" au "viumbe vitakatifu"

Psalms 89:7

Yeye ni Mungu anayetukuzwa sana katika baraza la watakatifu

"Baraza la watakatifu lamtukuza sana Mungu"

baraza la watakatifu

"mkusanyiko wa viumbe wa mbinguni" au "mkusanyiko wa malaika"

nani mwenye nguvu kama wewe, Yahwe?

Mwandishi anauliza hili swali kusisitiza kuwa hakuna mtu mwenye nguvu kama Yahwe.

Ukweli wako unakuzunguka

Yahwe kufanya kile alichoahidi kufanya inazungumziwa kana kwamba ukweli wake ni joho au nguo inayozungushwa kwake.

Psalms 89:9

Unatawala bahari lenye hasira kali

"Una madaraka na bahari lenye hasira kali"

Ulimponda Rahabu kama mtu aliyeuawa

Neno "Rahabu" hapa linamaanisha mnyama mkubwa wa baharini.

kwa mkono wako imara

Hapa "mkono" inawakilisha uwezo. "kwa uwezo wako mkuu"

Psalms 89:11

kaskazini na kusini

Mwandishi anatumia maneno "kaskazini" na "kusini" kwa pamoja kumaanisha kuwa Mungu aliumba kila kitu kila sehemu.

Tabori na Hermoni wanafurahi katika jina lako

Tabori ni mlima kusini magharibi mwa bahari la Galilaya na Hermoni ni mlima kaskazini mashariki mwa bahari la Galilaya. Mwandishi anaelezea milima hii kana kwamba ni watu wanaoweza kufurahi. "Ni kana kwamba mlima Tabori na mlima Hermoni ilikuwa ikifurahi katika jina lako"

katika jina lako

Hapa "jina" linamaanisha mtu mzima. "katika wewe"

Psalms 89:13

Una mkono wenye uweza na mkono imara, na mkono wako wa kuume uko juu

Maneno "mkno wenye uweza," "mkono imara," na "mkono wa kuume" yote inawakilisha nguvu ya Mungu.

mkono wako wa kuume uko juu

Kuinua mkono wa kuume angani ni ishara inayoonesha nguvu.

Haki na hukumu ni msingi wa kiti chako cha enzi

Mungu kutawala kama mfalme na kufanya kilicho sawa na haki inazungumziwa kana kwamba kiti cha enzi cha Mungu ni jengo, na haki na hukumu ndio msingi wake.

kiti chako cha enzi

Kiti cha enzi kinawakilisha utawala wa Mungu kama mfalme.

Uaminifu wa agano na uaminifu unakuja mbele zako

Mungu kuwa mwaminifu daima na kufanya alichoahidi kufanya inazungumziwa kana kwamba uaminifu wa agano na uaminifu huja pamoja na kukutana na Mungu.

Psalms 89:15

wanao kuabudu

Hapa neno "kuabudu" inaashiria kupiga kelele na kupuliza pembe. Haya yalikuwa matendo ya kawaida wa kuabudu wakati wa sikukuu za Waisraeli.

wanatembea

Hapa watu kuishi maisha yao inazungumziwa kana kwamba wanatembea.

katika mwanga wa uso wako

Mwandishi anazumzungumzia Yahwe kuwatendea fadhila kana kwamba uso wa Yahwe ulimulika mwanga kwao. "wakijua kuwa unawatendea fadhila"

katika jina lako

Hapa "jina" linamwakilisha mtu. "katika wewe"

katika haki yako wanakutukuza

"wanakutukuza kwa sababu daima huwa unafanya kilicho sawa"

Psalms 89:17

Wewe ni nguvu yao ya fahari

"Wewe huwafanya kuwa na nguvu ya ajabu"

Wewe ni nguvu yao

Hapa "yao" inamaanisha Waisraeli. Mwandishi angejiweka pamoja kama mmoja wa Waisraeli. "Wewe ni nguvu yetu"

sisi ni washindi

Hapa "sisi" inamaanisha mwandishi na Waisraeli.

Kwa kuwa ngao yetu ni ya Yahwe

Mfalme ambaye huwalinda watu wake na ambaye Yahwe amemchagua anazungumziwa kana kwamba ni ngao ya Yahwe.

Psalms 89:19

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anachukulia kuwa msomaji anafahamu historia ya jinsi Daudi alivyochaguliwa kuwa mfalme.

Nimeweka taji kwa aliye hodari

Kuweka taji juu ya kichwa cha mtu ni ishara ya kumfanya kuwa mfalme. "Nimemfanya mtu hodari kuwa mfalme"

Nimeweka taji kwa aliye hodari

Tafsiri zingine za Biblia zina "kumpa nguvu aliye hodari" au "kumsaidia aliye hodari."

Nimemwinua mmoja niliyemchagua miongoni mwa watu

Hapa "nimemwinua" inamaanisha kuchagua. Inadokezwa kuwa Mungu alimchagua mtu huyu kuwa mfalme. "Nimemchagua mmoja miongoni mwa watu kuwa mfalme"

kwa mafuta yangu matakatifu nimempaka

Hapa kumwaga mafuta juu ya kichwa cha mtu ni ishara kuwa Mungu anamchagua huyo mtu kuwa mfalme.

Mkono wangu utamshika; mkono wangu utamtia nguvu

Hapa "mkono" unamaanisha nguvu na mamlaka ya Yahwe. "nitamshika na kumfanya kuwa na nguvu"

mwana wa uovu

Mwandishi anawazungumzia wale wenye sifa au tabia ya uovu kama "wana wa uovu." "mtu mwovu"

Psalms 89:24

Kauli Unganishi:

Yahwe anaendelea kumzungumzia Daudi.

Ukweli wangu na uaminifu wangu wa agano utakuwa naye

Mungu kuwa mwaminifu daima na kufanya alichomwahidi Daudi inazungumziwa kana kwamba ukweli na uaminifu ni vitu ambavyo vitakuwa na Daudi.

kwa jina langu atashinda

Hapa "jina" linawakilisha nguvu ya Mungu. "Mimi, Mungu, nitamsababisha awe na ushindi"

Nitaweka mkono wake juu ya bahari na mkono wake wa kuume juu ya mito

Hapa "mkono" na "mkono wake wa kuume" inawakilisha uwezo na mamlaka, Hapa "bahari" inaonekana kumaanisha bahari ya Kati magharibi mwa Israeli, na "mito" inamaanisha mto Frati ulio mashariki. Hii inamaanisha kuwa Daudi atakuwa na mamlaka juu kila kitu kutoka baharini hadi kwenye mto. "Nitampa mamlaka juu ya kila kitu kutoka bahari ya Kati hadi mto Frati"

Ataniita, 'Wewe ni baba yangu, Mungu wangu, na mwamba wa wokovu wangu'

Hii ina nukuu ndani ya nukuu. "Atasema kuwa mimi ni baba yake, Mungu wake, na mwamba wa wokovu wake"

mwamba wa wokovu wangu

Yahwe kumlinda na kumwokoa daudi inazungumziwa kana kwamba Yahwe ni mwamba wa juu ambao Daudi aliweza kusimama juu yake kwa ajili ya ulinzi kutoka kwa adui.

Psalms 89:27

Kauli Unganishi:

Yahwe anaendelea kumzungumzia Daudi.

Pia nitamweka kama mzaliwa wa kwanza

Yahwe kumpa Daudi cheo maalumu na faida zaidi ya watu wengine wote inazungumziwa kana kwamba Daudi atakuwa mzaliwa wa kwanza wa Yahwe.

kiti cha cha enzi cha kudumu kama anga zilizo juu

Mtu kutoka familia ya Daudi kutawala daima kama mfalme inazungumziwa kana kwamba kiti chake cha enzi kitadumu muda sawa kama anga itakavyodumu.

kiti cha cha enzi

Hapa "kiti cha enzi" kinawakilisha uwezo wa kutawala kama mfalme.

Psalms 89:30

watoto wake

"uzao wa Daudi"

nitaadhibu uasi wao kwa fimbo

Mungu kuadhibu uzao wa Daudi inazungumziwa kana kwamba atawapiga kwa fimbo. "nitawaadhibu kwa kuasi dhidi yangu"

na udhalimu wao kwa mapigo

Mungu kuadhibu uzao wa Daudi inazungumziwa kana kwamba Mungu atawapiga kiuhalisia. "na nitawaadhibu kwa sababu wametenda dhambi dhidi yangu"

Psalms 89:33

Sitaondoa upendo wangu thabiti kutoka kwake wale kutokuwa mwaminifu kwa ahadi yangu

"Daima nitampenda Daudi, na nitafanya nilichomwahidi"

maneno ya midomo yangu

Hapa "maneno" yanawakilisha alichosema. Pia "midomo" inawakilisha mdomo wote na mtu anayezungumza. "nilichosema"

Psalms 89:35

Nimeapa kwa utakatifu wangu

Yahwe anatumia utakatifu wake kama msingi wa kiapo chake. Hii ni njia ya kuhakikisha kuwa hakika atafanya alichoahidi kufanya.

na kiti chake cha enzi kitakuwa kama jua mbele yangu

"na kiti chake cha enzi kitaendelea kama jua mbele yake"

kiti chake cha enzi

Hapa "kiti cha enzi" kinawakilisha uwezo wa kutawala kama mfalme. Mungu anaahidi kuwa mmoja wa uzao wa Daudi daima atakuwa mfalme.

kama jua mbele yangu

Mungu anafananisha utawala wa Daudi kama mfalme na jua kusisitiza kuwa mtu kutoka uzao wa Daudi atatawala daima kama mfalme.

kitaimarishwa milele

Hapa kinachozungumziwa ni kiti cha enzi au uwezo wa kutawala kama mfalme. "nitakisababisha kudumu milele"

milele kama mwezi

Mungu anafananisha utawala wa Daudi kama mfalme na mwezi kusisitiza kuwa mtu kutoka uzao wa Daudi atatawala daima kama mfalme.

mwezi, shahidi wa uaminifu wa angani

Mwezi unazungumziwa kana kwamba ni mtu anayeshuhudia Mungu akifanya ahadi yake kwa Daudi. "mwezi, ambao ni kama shahidi mwaminifu aliye angani"

Sela

Hili linaweza kuwa neno la kimuziki linalowaongoza watu jinsi ya kuimba au kujecheza vyombo hapa. Tafsiri zingine huandika neno hili la Kiebrania, na zingine haziliweki.

Psalms 89:38

umekatata na kutupa

"umemkataa na kumtupa mfalme"

na mfalme wako mtiwa mafuta

"na mfalme uliye mchagua"

Umekanusha agano la mtumishi wako

"Umelikataa agano"

umetia najisi taji lake ardhini

Kusukuma ardhini au mavumbini ni ishara ya aibu kubwa. "umetia najisi taji lake ardhini" au "Umesababisha taji lake kuanguka mavumbini"

taji lake

Hii inawakilishwa uwezo wa mfalme kama mfalme na haki yake ya kutawala.

Umevunja chini kuta zake zote. Umeharibu ngome zake

Hii inadokeza kuwa Mungu aliwaruhusu adui zake kuangamiza ulinzi wa Yerusalemu. "Umewaruhusu adui kuvunja chini kuta na kuharibu ngome katika Yerusalemu"

Psalms 89:41

kwa majirani zake

Hapa "majirani" inamaanisha watu mataifa ya karibu.

Umeinua mkono wa kuume wa adui zake

Hapa "mkono wa kuume" unawakilisha uwezo. "Kuinua mkono wa kuume" inamaanisha kuwa Yahwe aliwafanya adui zake kuwa na nguvu ya kutosha ya kumshinda mfalme aliye chaguliwa na Mungu.

geuza nyuma makali ya upanga wake

Hapa "upanga" unawakilisha nguvu ya mfalme vitani. Kugeuza upanga inawakilisha kumfanya mfalme kushindwa kushinda vitani.

makali ya upanga wake

Hapa "makali" inawakilisha upanga wote. "upanga wake"

hujamfanya asimame wakati akiwa vitani

Hapa "asimame" inawakilisha kuwa mshindi vitani. "Hujamsaidia kuwa mshindi vitani"

Psalms 89:44

umeleta chini kiti chakecha enzi hadi ardhini

Hapa "kiti cha enzi" kinawakilisha uwezo wa kutawala kama mfalme. "wewe, Yahwe, umemaliza utawala wake kama mfalme"

Umefupisha siku zake za ujana

Hii ni njia ya kusema Mungu alimfanya mfalme kuonekana mzee wakati alikuwa bado ni kijana. "Hata wakati bado ni kijana umemfanya kuwa mnyonge kama mzee"

umemfunika na aibu

Yahwe kumwaibisha kabisa mfalme inazungumziwa kana kwamba aibu ni vazi ambalo Mungu alitumia kumfunika mfalme.

Psalms 89:46

Hadi lini, Yahwe? Utajificha, milele?

Mwandishi anatumia maswali haya kusisitiza kuwa hataki Mungu aendelee kumkataa mfalme. "Tafadhali, Yahwe, usikatae kumsaidia mfalme milele."

Utajificha

Mungu kutomsaidia mfalme inazungumziwa kana kwamba Mungu alikuwa anajificha kwake. "Je! Utakataa kumsaidia mfalme"

Hadi lini hasira yako itawaka kama moto?

Mwandishi anatumia swali kusisitiza kuwa hataki Mungu aendelee kubaki na hasira. "Tafadhali usiendelee kuwa na hasira"

hasira yako itawaka kama moto

Mungu kuwa na hasira sana inazungumziwa kana kwamba hasira yake ilikuwa moto mkali.

kwa ubatili gani umewaumba watoto wote wa mwanadamu

"kwamba umewaumba watu wote kufa kibatili"

watoto wote wa mwanadamu

Hii inamaanisha wanadamu kwa ujumla. "wanadamu" au "watu"

Nani anaweza kuishi na asife, au kuokoa maisha yake mwenyewe kutoka katika mkono wa kuzimu?

Mwandishi anatumia maswali haya kusisitiza kuwa watu wote watakufa. "Hakuna mtu anayeweza kuishi milele au kujifufua baada ya kufa"

kuokoa maisha yake mwenyewe kutoka katika mkono wa kuzimu

Hapa "mkono" unamaanisha uwezo. Mwandishi anazungumzia kuzimu kana kwamba ni mtu aliye na nguvu juu ya wale waliokufa. Maana zinazowezekana ni 1) mtu hawezi kujifufua baada ya kufa au 2) mtu hawezi kujizuia kufa.

Psalms 89:49

Bwana, yako wapi matendo yako ya kale ya uaminifu wako wa agano ulioahidi kwa Daudi katika ukweli wako?

Mwandishi anatumia swali kumwomba Bwana kuwa mwaminifu kwa agano lake na Daudi. "Bwana, kuwa mwaminifu kwa agano lako na Daudi kama ulivyokuwa kipindi cha nyuma"

Ita akilini

Mwandishi anamwomba Mungu kuleta hili katika kumbukumbu yake. "Kumbuka" au "Zingatia"

kejeli iliyolengwa kwa watumishi wako

Hapa "watumishi wako" inamaanisha watu wa Israeli. "jinsi wanavyotukejeli, watumishi wako"

jinsi ninavyobeba moyoni mwangu matusi mengi sana kutoka kwa mataifa

Hapa "moyo" unawakilisha hisia za mtu. "Ninavumilia matusi mengi sana kutoka kwa watu wa mataifa" au " Ninateseka kwa sababu watu wa mataifa wananitukana"

kutoka kwa mataifa

Hapa "mataifa" inawakilisha watu wa mataifa.

Adui zako wanatupa matusi

Adui kupiga kelele za matusi kwa mfalme inazungumziwa kana kwamba matusi ni kitu ambacho adui wanamtupia mfalme kwa nguvu.

wanakejeli hatua za watiwa mafuta wako

Hapa "hatua" inawakilisha pale ambapo mfalme anaenda. "wanamkejeli mtiwa mafuta wako popote aendapo"

Psalms 89:52

Taarifa ya Jumla:

Mstari huu ni zaidi ya mwisho wa zaburi hii. Ni kauli ya kufunga ya kitabu kizima cha 3 cha Zaburi, ambacho kinaanza katika Zaburi 73 na kuishia na Zaburi 89.

Abarikiwe Yahwe milele

"Watu wamsifu Yahwe milele"

Amina na Amina

Neno "Amina" linarudiwa kusisitiza kukubali kilichosemwa.

Psalms 90

Psalms 90:1

Taarifa ya Jumala:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Ombi la Musa

"Hili ni ombi ambalo Musa aliandika"

Bwana, umekuwa kimbilio letu

Mungu kuwalinda watu wake inazungumziwa kana kwamba Mungu alikuwa kimbilio au kivuli. "Bwana, umekuwa kama kivuli kwa ajili yetu"

katika vizazi vyote

"daima"

Kabla milima haijaumbwa

"Kabla hujaumba milima"

umbwa

"tengeneza"

dunia

Hii inawakilisha kila kitu kilichomo duniani.

kutoka milele hadi milele

Msemo huu unawakilisha muda wote wa zamani, wa sasa, na wa baadaye.

Psalms 90:3

Unamrudisha mtu mavumbini

Hii inadokezwa kuwa kama jinsi Mungu alivyoumba binadamu wa kwanza, Adamu, kutoka mavumbini, Mungu atasababisha miili ya watu kurudi mavumbini baada ya kufa. "Unawarudisha watu kwenye mavumbi wanapokufa"

Unamrudisha mtu

Hapa "mtu" inamaanisha watu kwa ujumla.

Rudini, nyie uzao

"Rudini mavumbini, nyie uzao" au "Rudini kwenye mchanga, nyie uzao"

nyie uzao wa wanadamu

Hii ni njia ya kumaanisha watu kwa ujumla. "nyie wanadamu" au "nyie watu"

Kwa kuwa miaka elfu moja machoni pako ni kama siku ya jana inavyopita, na kama kesha la usiku

Mwandishi anamaanisha kuwa kipindi kirefu cha muda kinaonekana kama kipindi kifupi kwa Mungu. "Unaona miaka elfu moja sawa na siku moja ya nyuma, au kama masaa machache ya usiku" au "Hata miaka elfu moja sio muda mrefu kwako"

miaka elfu moja

"miaka 1,000"

machoni pako

Hapa "machoni" inawakilisha mawazo. "kwako"

Psalms 90:5

Unawafagia kama na mafuriko wanapolala

Mungu kuwasababisha watu kufa kabla inazungumziwa kana kwamba aliwafagia na mfagio. Kufagia huku pia kunazungumziwa kana kwamba ni mafuriko yaliyowabeba watu. "Bwana, unawaangamiza watu kama na mafuriko na wanakufa"

wanapolala

Hii ni jia ya ya ustarabu ya kuzungumzia watu kufa.

asubuhi ni kama nyasi ... jioni linanyauka na kukauka

Watu wanafananishwa na nyasi kusisitiza kuwa watu hawaishi muda mrefu sana.

linachanua na kuota

Misemo hii miwli inamaanisha jinsi nyasi zinavyoota. "linaanza kuota na kukua"

linanyauka na kukauka

Misemo hii miwili inamaanisha jinsi nyasi zinavyokufa. "linafifia na kukauka"

Psalms 90:7

tumemezwa katika hasira yako

Mungu kuwaangamiza watu katika hasira yake inazungumziwa kana kwamba hasira ya Mungu ni moto unaowaunguza kabisa watu. "Unatuangamiza katika hasira yako"

na katika gadhabuyako tunaogopa

"na unapokasirika tunaogopa sana"

Umeweka udhalimu wetumbele zako, dhambi zetu zilizofichwa katika nuru ya uwepo wako

Mungu kuzingatia dhambi za watu inazungumziwa kana kwamba dhambi ni vitu anavyoweza kuweka mbele yake na kuzitazama. "Unaona kila kitu kiovu tunachofanya, hata vitu vya dhambi tunavyofanya sirini"

Psalms 90:9

Maisha yetu yanapita chini ya gadhabu yako

"Maisha yetu yanafika mwisho kwa sababu ya gadhabu yako"

kama kite

Mwandishi anafananisha maisha ya mtu na kite kusisitiza kuwa maisha ni mafupi sana.

sabini

"70"

themanini

"80"

hata miaka yetu mizuri yana alama ya taabu na huzuni

"Hata katika miaka yetu mizuri tunapitia taabu na huzuni"

tunapaa

Hii ni njia ya ustaarabu ya kusema watu wanaokufa.

Psalms 90:11

Nani ajuaye ukali wa hasira yako, na gadhabu yako ambayo inalingana na kukucha wewe?

Mwandishi anatumia swali kusisitiza kuwa hakuna mtu aliyepitia kikamilifu hasira ya Mungu. Kwa hiyo hakuna mtu anayemheshimu Mungu na kuogopa hasira yake watu wanapotenda dhambi. "Hakuna mtu anayejua ukali wa hasira yako. Kwa hiyo hakuna mtu anayeogopa gadhabu yako wanapotenda dhambi."

Geuka, Yahwe! Hadi lini?

Kumwomba Yahwe kutokuwa na hasira tena inazungumziwa kana kwamba mwandishi anataka Mungu ageuke kimwili kutoka katika hasira yake. "Yahwe, tafadhali usiwe na hasira na sisi tena'

Hadi lini?

Mwandishi anatumia swali kueleza kuwa anataka Mungu aache kuwa na hasira.

Kuwa na huruma kwa watumishi wako

Hapa "watumishi wako" inamaanisha watu wa Israeli. "Kuwa na huruma kwetu, watumishi wako"

Psalms 90:14

Turidhishe asubuhi

"Turudhishe kila asubuhi"

na uaminifu wako wa agano

"kwa kuwa mwaminifu kwa sababu ya agano lako na sisi"

kwa kulingana na siku ulizotutesa na kwa miaka tuliyopitia taabu

Misemo yote hii miwili inamaanisha kitu kimoja. Mwandishi anamwomba Yahwe kuwafanya kuwa na furaha kwa kisai kile kile cha muda alichowaadhibu. "kwa kiasi sawa cha muda ulichotuumiza na kutusababisha kuteseka"

Acha watumishi wako

Hapa "watumishi wako" inamaanisha watu wa Israeli. "Acha sisi, watumishi wako" au "Acha sisi"

acha watoto wako

Hapa "watoto" inamaanisha watoto na uzao.

waone fahari yako

"waone mambo makuu unayoyafanya"

Psalms 90:17

Na fadhila ya Bwana Mungu wetu iwe yetu

"Na Bwana Mungu wetu awe na huruma kwetu"

fanikisha kazi ya mikono yetu

Hapa "mikono" inawakilisha mtu mzima. "tusababishe tufanikiwe"

Psalms 91

Psalms 91:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Yeye anayeishi ... atabaki ... ya Mwenyezi

"Aliye juu, Mwenyezi, atawajali wote wanaoishi mahali anapoweza kuwalinda"

anayeishi katika kivuli cha Aliye juu

Neno "kivuli" ni sitiari ya ulinzi. "anayeishi mahali ambapo Aliye juu humlinda"

Aliye juu

Maneno "Aliye juu" yanamaanisha Yahwe.

atabaki katika kivuli cha Mwenyezi

Neno "kivuli" hapa ni sitiari ya ulinzi. "atabaki mahali ambapo Mwenyezi anaweza kumlinda"

Mwenyezi

yule mwenye uwezo na mamlaka juu ya kila kitu

Nitasema ya Yahwe

"Nitasema kumhusu Yahwe"

kimbilio lnagu na ngome yangu

"Kimbilio" ni sehemu ambapo mtu anaweza kwenda na kuwa na mtu au kitu kinachomlinda. "Ngome" ni kitu ambacho watu hutengeneza ili wajilinde wao na mali zao. Asafu anayatumia hapa kama sitiari ya ulinzi. "yule ambaye ninaweza kwenda kwake na atanilinda"

Psalms 91:3

Kwa kuwa atakuokoa kutoka katika mtego wa mwindaji na kutoka katika tauni hatari

"Kwa kuwa Mungu atakuokoa kutoka katika mtego wa mwindaji na atakuokoa kutoka katika tauni zinazoweza kuua"

mtego wa mwindaji

"kutoka katika mtego ambao mwindaji aliweka kukushika"

Atakufunika kwa mbawa zake, na chini ya mbawa zake utapata kimbilio

Ulinzi wa Mungu hapa unazungumziwa kama "mbawa" ambazo ndege hutumia kufunika makinda yake dhidi ya hatari. "Atakufunika na mbwa zake" na "chini ya mbawa zake" zina maana moja. "Atakuweka salama na atakulinda"

Uaminifu wake ni ngao na ulinzi

Uaminifu wa Mungu hapa unazungumziwa kama "ngao" ambayo inaweza kuwalinda watu wanaomtegemea. "Unaweza kumtumaini akulinde"

ulinzi

Hakuna mtu anayejua kwa uhakika maana ya neno hili. Maana zinazowezekana ni 1) ngao ndogo iliyofungwa kwenye mkono wa askari inayotumika kujilinda dhidi ya mishale na panga au 2) ukuta wa mawe uliowekwa katika duara ambayo askari wanaweza kujificha na kupiga mishale.

Psalms 91:5

hofu wakati wa usiku

Mwandishi anazungumzia "hofu" kana kwamba ni roho au mnyama mkali ambaye anaweza kushambulia usiku na kuwatisha watu. "vitu vitakushambulia usiku"

wakati wa usiku ... mchana

Misemo hii miwli imewekwa pamoja kumaanisha nyakati zote zinazowezekana za usiku na mchana.

mshale unaopaa mchana

"Mshale" ni njia nyingine ya kusema watu wanaopiga mishale. "watu wanao kushambulia kwa mishale mchana"

au tauni inayozurura

Mwandishi wa zaburi anazungumzia ugonjwa kana kwamba ni mtu aliyetoka usiku na kuua watu wengine. "Hautaogopa kufa kutokana na ugonjwa"

inayozurura

anayeenda popote atakapoa kwenda na wakati wowote

gizani ... mchana

Misemo hii miwli imewekwa pamoja kumaanisha nyakati zote zinazowezekana za usiku na mchana.

ugonjwa

ugonjwa unaowafanya watu kuuguwa kwa wakati mmoja

Watu elfu wanaweza kuanguka katika upande wako na elfu kumi katika mkono wako wa kuume

"Watu wengi wanaweza kuanguka pembeni yetu."

haitakufikia

"uovu hauta kudhuru"

Psalms 91:8

Utatazama na kuona

"Wewe mwenyewe hautateseka, lakini utatazama kwa makini, na utaona"

adhabu ya waovu

"jinsi Mungu anvyowaadhibu waovu"

Yahwe ni kimbilio langu

"Yahwe ndiye ninayemfuata ninapohitaji mtu wa kunilinda"

Mfanye Aliye juu kimbilio lako pia

"Unapaswa kumfanya Aliye juu awe kimbilio lako pia." Mwandishi anaacha kuzungumza na Mungu na anaanza kuzungumza na msomaji.

Psalms 91:10

Hakuna uovu utakaokupita

"Hakuna kitu kiovu kitakachotokea kwako"

hakuna mateso yatakayo kuja karibu na nyumba yako

Mwandishi anawazungumzia watu wanaowatesa wengine kana kwamba walikuwa ndio madhara waliyoyasababisha. "hakuna mtu atakayeweza kudhuru familia yako"

Kwa kuwa atawaongoza

"Yahwe ataamuru"

katika njia zako zote

Mwandishi anazungumzia jinsi mtu anavyoishi kana kwamba ni njia ambayo mtu alitembea. "katika kila kitu unachofanya" au "wakati wote'

Psalms 91:12

Watakuinua

"Malaika wa Yahwe watakuinua"

hautajikwaa mguu wako kwenye jiwe

Malaika hawatalinda mguu wa msomaji pekee bali na mwili wake mzima. "hautaogonga mguu wako kwenye jiwe" au "hakuna kitu kibaya kitakachotokea kwako"

Utawaponda simba na vifutu chini ya miguu yako; utakanyaga juu ya simba wadogo na nyoka

Ambapo "atajikwaa mguu wako kwenye jiwe" ni tatizo dogo, simba na nyoka ni mnifano ya hatari kubwa. Mwandishi anazungumzia zimba na nyoka kana kwamba walikuwa ni wadogo ya kutosha kukanyagwa chini ya mguu wa mtu. "Utaweza kuwaua simba na nyoka kana kwamba ni wanyama wadogo ambao unaweza kuwakanyaga chini ya miguu yako"

vifutu

aina ya nyoka wenye sumu.

kanyaga

kuponda kwa kutembea kwa nguvu

Psalms 91:14

Kwa sabau amejitoa kwangu

"Kwa sababu ananipenda mimi"

Nitakuwa naye katika taabu

"Nitakuwa naye wakati yuko katika taabu"

nitampa ushindi

"nitamwezesha kuwashinda adui zake"

nitamridhisha na maisha marefu

Mwandishi anazungumzia maisha kana kwamba ni kitu ambacho mtu anaweza kula. Nitamruhusu kuishi maisha marefu na yenye furaha"

na kumwonesha wokovu wangu

"na nitamwonesha wokovu wangu." Mwandishi wa zaburi anazungumzia kazi ambayo Mungu hufanya kuwaokoa watu kana kwamba ni kitu chenye umbo. "Nitamwokoa ili ajue kuwa mimi ndiye niliyemwokoa"

Psalms 92

Psalms 92:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

kuimba sifa kwa jina lako

Maneno "jina lako" ni njia nyingine ya kusema "wewe." "kuimba sifa kwako"

kutangaza uaminifu wako wa agano

"kuwaambia watu kuwa wewe ni mwaminifu kutunza agano alko"

ukweli wako

"kuwa kila kitu unachosema ni kweli"

Psalms 92:4

furaha

furaha"

kupitia matendo yako

"kwa kile ulichofanya"

matendo ya mikono yako

Neno "mikono" ni njia nyingine ya kumaanisha mtu mzima. "Kile ulichofanya"

matendo yako

"kile ulichofanya"

Mawazo yako ni marefu sana

"Hatuwezi kuelewa unachopanga kufanya hadi ukifanye"

Mawazo yako

"Unachowaza" au "Unachopanga"

Psalms 92:6

katili

"mwenye vurugu na mjinga"

Wakati waovu wanpochipuka kama nyasi

Hii inafananisha watu waovu na nyasi, ambayo huota upesi na sehemu nyingi. "Wakati watu waovu wanapotokea haraka na kuonekana kuwa kila sehemu, kama nyasi"

wamehukumiwa kwa kuangamizwa milele

"Mungu ameamua kuwa atawaangamiza kabisa"

Psalms 92:8

Hakika, watazame adui zako, Yahwe

Maandishi mengi hayana maneno haya.

Wataangamia

"Watakufa" au "Utawaua"

Wale wote wanaofanya maovu watatawanywa

"utawatawanya wote wanaofanya uovu"

watatawanywa

Maandishi mengi yameandikwa, "wametawanywa."

watatawanywa

"wataondolewa"

Psalms 92:10

Umeinua pembe langu kama pembe la nyati

Mwandishi wa zaburi anamzungumzia Mungu kana kwamba Mungu amemfanya kuwa na nguvu kama mnyama wa porini. "Umenifanya kuwa na nguvu kama nyati"

Umeinua ... pembe

"Umenifanya kuwa na nguvu"

Nimetiwa mafuta na mafuta mapya

Maana zinazowezekana ni kwamba mafuta ambayo Mungu ameweka juu ya mwandishi wa zaburi ni sitiari ya Mungu 1) kufanya kuwa mwenye furaha, "umenifanya kuwa na furaha sana" au 2) kumfanya kuwa na nguvu, "umenifanya kuwa na nguvu" au 3) kumwezesha kuwashinda adui zake, "umeniwezesha kuwashinda adui zangu."

Macho yangu yameona anguko la adui zangu; masikio yangu yamesikia maangamizi ya adui zangu waovu

Maneno "macho" na "masikio" ni njia nyingine ya kumaanisha mtu anayesikia na kuona. "Nimeona na kusikia kuhusu kushindwa kwa adui zangu waovu"

Psalms 92:12

Wenye haki watastawi kama mtende

Maana zinazowezekana ni kwamba watu wenye haki watakuwa kama mtende wenye afya kwa sababu 1) watakuwa imara au 2) wataishi muda mrefu.

wataota kama mti wa seda ya Lebanoni

Maana zinazowezekana no kwamba watu wenye haki watakuwa kama mti wa seda unaoota katika nchi ya Lebanoni kwa sababu 1) watakuwa imara au 2) watu watawaheshimu.

Wamepandwa

"Yahwe amewapanda" au "Yahwe anawatunza kana kwamba ni miti aliyoipanda"

katika nyumba ya Yahwe ... katika nyua za Mungu wetu

Mwandishi wa zaburi anawazungumzia watu wanaomwabudu Mungu kwa ukweli kana kwamba walikuwa miti inayoota katika nyumba ya Yahwe.

wanastawi

Mwandishi wa zaburi anawazungumzia watu wenye haki kana kwamba ni miti yenye afya. "wanakua vizuri" au "wana nguvu sana"

katika nyua za Mungu wetu

katika baraza la hekalu Yerusalemu.

Psalms 92:14

Wanazaa matunda

Mwandishi anawazungumzia watu wenye haki kana kwamba walikuwa miti ambayo inatoa matunda. "Wanampendeza Mungu"

wanabaki na ubichi na kijani

Mwandishi anawazungumzia watu wenye haki kana kwamba walikuwa miti. "wanabaki imara na wenye afya" au "huwa wanafanya kinachompendeza Mungu"

kijani, kutangaza kwamba

Maana zinazowezekana ni 1) kijani, ili watangaze" au 2) "kijani. Hii inaonesha kwamba"

Yeye ni mwamba wangu

"Yahwe ndiye anayenilinda." Mwandishi wa zaburi anamzungumzia Yahwe kana kwamba ni mwamba ambao utamlinda.

Psalms 93

Psalms 93:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

amevikwa na adhama; Yahwe amemvika na kujifunga na nguvu

Mwandishi wa zaburi anazungumzia nguvu ya Yahwe na adhama yake kana kwamba vilikuwa vitu ambavyo Yahwe alivaa. "anawaonesha wote kuwa ni mfalme mwenye uwezo" au "adhama yake ipo kwa ajili ya kila mtu kuona, kama joho ambalo mfalme huvaa; kila kitu kumhusu Yahwe kinaonesha kuwa ana nguvu na yuko tayari kufanya kazi kubwa"

adhama

uwezo wa mfalme na jinsi mfalme anavyotenda

kujifunga

kufunga mshipi — ukanda wa ngozi au kitu kingine ambacho mtu huvaa kiunoni — kujianda kwa ajili ya kazi au mapambano

Dunia imewekwa imara

Hii inaweza kuelezwa kwatika hali ya kutenda. "Umeiweka imara dunia"

haiwezi kusogezwa

Hii inaweza kuelezwa kwatika hali ya kutenda. "hakuna atakaye isogeza"

Kiti chako cha enzi kimewekwa tangu nyakati za kale

Hii inaweza kuelezwa kwatika hali ya kutenda. "Ulikiweka kiti chako cha enzi tangu nyakati za kale"

wewe ni tangu milele

"ulikuwepo siku zote"

Psalms 93:3

bahari ... bahari

Tafsiri zingine zinasoma "mafuriko ... mafuriko." Neno hili mara nyingi humaanisha mto, lakini "bahari ... bahari" limechaguliwa hapa kwa sababu mabahari, na sio mito, huwa ina "mawimbi" yenye "kishindo na kuunguruma."

zimeinua sauti zao; mawimbi ya bahari ya kishindo na kuunguruma

Mwandishi wa zaburi anazungumzia bahari kana kwamba ni mtu anayeweza kuzungumza. "zimefanya sauti kuu kwa sababu mawimbo yao yana kishindo na kuunguruma"

kuunguruma

kupaza sauti ndefu ya kelele.

Juu ya vishindo vya mawimbi mengi, mawimbi makubwa yaumkayo ya bahari

Msemo huu "wavunjaji wakuu wa bahari" inamaana moja na "mawimbi mengi" na inasisitiza jinsi mawimbi yalivyo. "Juu ya vishindo vya mawimbi makubwa ya baharini"

mawimbi makubwa yaumkayo

mawimbi makubwa yajayo kwenye nchi

Aliye juu

Mwandishi wa zaburi anazungumzia mahali anapoishi Mungu kana kwamba palikuwa juu ya nchi. "mbinguni"

Psalms 93:5

makini

kuwa wa dhati

ni zakuaminika sana

"daima zinabaki hivyo hivyo" au "hazibadiliki"

utakatifu unapamba nyumba yako

Mwandishi wa zaburi anazungumzia nyumba ya Yahwe kana kwamba ilikuwa ni mwanamke aliyevaa nguo nzuri au mapambo ya vito na utakatifu wa Yahwe kama zile nguo nzuri na mapambo ya vito. "nyumba yako ni nzuri kwa sababu wewe ni mtakatifu" au "utakatifu wako unaifanya nyumba yako kuwa nzuri kama nguo nzuri na mapambo ya vito yanavyomfanya mwanamke kuwa mzuri zaidi"

nyumba yako

hekalu liliko Yerusalemu

unapamba

unafanya kuwa nzuri

Psalms 94

Psalms 94:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

ng'aa juu yetu

"jioneshe" au "dhihirisha hukumu yako"

Inuka, mwamuzi wa ulimwengu, wape walio na kiburi wanachostahili

"Njoo, mwamuzi wa ulimwengu, na uwaadhibu wenye kiburi"

Inuka

Mwandishi wa zaburi anazungumzia kuanza kufanya kitu kama kuinuka. "Chukua hatua" au "Fanya kitu"

Psalms 94:3

Hadi lini waovu, Yahwe, hadi lini waovu watashangilia?

Mwandishi wa zaburi anarudia wali kuonesha kuwa hana furaha na muda ambao Yahwe amewaruhusu waovu washangilie. "Umesubiri muda mrefu sana Yahwe; umesubiri muda mrefu sana kuwazuia waovu kushangilia."

waovu watashangilia

"Je! Waovu watashangilia kwa sababu huwaadhibu kwa matendo maovu wanayofanya"

Wanamwaga

"Wale wote wanaofanya uovu wanamwaga"

Wanamwaga nje maneno yao kiburi

Mwandishi wa zaburi anaandika kuhusu waovu kuzungumza kana kwamba maneno yao yalikuwa kimiminiko kinachomwagwa nje.

wale wote wanaofanya majivuno ya uovu

"Wale wote wanaofanya uovu wanajisifu juu ya matendo yao ya uovu na tabia zao"

Psalms 94:5

wanalitesa taifa

Hapa "taifa" linamaanisha watu wa hilo taifa. "wanawatesa watu wa taifa"

Wanawaponda

Mwandishi anawazungumzia watu wenye uwezo kuwatenda vibaya watu wanyonge kana kwamba ilikuwa kuwaponda au kuwabomoa katika vipande. "Wanawaangamiza kabisa" au "Wanawadhuru sana."

mjane

"wanawake ambao waume zao wamekufa"

wasio na baba

"watoto bila baba"

Mungu wa Yakobo hagundui

"Mungu wa Israeli haoni tunachokifanya"

Psalms 94:8

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi sasa anawaeleza watu waovu.

mtajifunza lini?

Swali hili la balagha linasisitiza hasira ya mwandishi na watu waovu anaozungumza nao. "acheni jia zenu za kipumbavu!" au "jifunzeni kutoka katika makosa yenu!"

Yeye aliyeumba sikio, je hasikii? Yeye aliyeumba jicho, hauoni?

Maswali haya balagha "Mungu aliumba masikio, kwa hiyo anaweza kusikia. Mungu aliumba macho, kwa hiyo anaweza kuona." au "Mungu aliumba masikio, kwa hiyo acheni kujifanya kana kwamba hasikii. Mungu aliumba macho, kwa hiyo acheni kujifanya kana kwamba haoni."

Psalms 94:10

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaendelea kuwaeleza watu waovu.

Yeye anayeyaadibu mataifa, je harekebishi?

Inadokezwa kuwa yahwe anawarekebisha watu wake. "Mnajua kuwa Yahwe huyarekebisha mataifa, kwa hiyo kuweni na uhakika kuwa atawarekebisha watu wake" au "atawaadhibu watu wake"

je harekebishi

Maana zinazowezekana ni 1) Mungu hurekebisha. "hurekebisha" au 2) Mungu huadhibu. "huadhibu"

kuwa ni mvuke

Hapa mawazo ya watu yanalinganishwa na mvuke unaopotea hewani. Hii ni sitiari inayoonesha jinsi wasivyo wa muhimu na wasivyo na faida.

mvuke

"umande"

Psalms 94:12

Taarifa ya Jumla:

Sasa mwandishi anazungumza na Yahwe tena.

hadi shimo lichimbwe kwa ajili ya waovu

Mwandishi anazungumzia yahwe kuwaadhibu waovu kana kwamba Yahwe anamtega mnyama shimoni. "hadi uchimbe shimo kwa ajili ya waovu" au "hadi uwaangamize waovu"

Psalms 94:14

urithi wake

"wale alio wachagua kuwa naye milele"

hukumu itakuwa ya haki tena

Mwandishi anawazungumzia wale wanaohukumu kana kwamba walikuwa ndiyo maamuzi wanayoyafanya. "waamuzi watahukumu tena kwa haki" au "waamuzi watafanya tena maamuzi ya haki"

wanyofu wa moyo

"wale ambao mioyo yao iko sawa na Mungu"

wanafuata

"watataka waamuzi wahukumu kwa haki"

Nani atainuka kunitetea mimi dhidi ya watenda maovu? Nani atasimama kwa ajili yangu dhi ya waovu

"Hakuna mtu atakaye nitetea dhidi ya watenda maovu. Hakuna mtu atakaye nisaidia kupigana dhidi ya waovu"

waovu

"watu waovu"

Psalms 94:17

Kama Yahwe asingekuwa msaada wangu ... ukimya

Hii ni hali ya kubuni. Yahwe alimsaidia, kwa hiyo hakuwa amelala katika sehemu ya ukimya.

Kama Yahwe asingekuwa msaada wangu

"Kama Yahwe asingenisaidia"

ningekuwa nimelala chini hivi punde kwenye sehemu ya ukimya

Hapa" ningekuwa nimelala chini" inamaanisha "mauti" na "sehemu ya ukimya" inamaanisha "kaburi." "katika muda mfupi, nitakuwa nimekufa, nikiwa nimelala kaburini"

Wasiwasi ndani yangu ukiwa mwingi, faraja zako hunifurahisha

Mwandishi anazungumzia wasiwasi kana kwamba anaweza kuhesabu kwa kutenganisha wasiwasi. "Ninapokuwa na wasiwasi kuhusu mambo mengi, umenifariji na kunifanya kuwa na furaha"

Psalms 94:20

Je! Kiti cha enzi cha uharibifu kinaweza kushirikiana na wewe, yule anayetengeneza udhalime kwa amri

Hili ni swali la balagha linalotumika kueleza wazo. "Linaweza kuelezwa kama kauli. "Mtawala mwovu anayeunda sheria zisizo za haki sio rafiki yako"

Kiti cha enzi cha uharibifu

Hapa "kiti cha enzi" kinawakilisha mfalme au mtawala. "mtawala mwovu" au "mwamuzi mwovu"

Wanapanga njama

kufanya mpango wa siri na mtu wa madhara au kitu kisicho halali

kuchukua maisha ya

Hii ni lahaja inayomaanisha kumuua mtu.

Psalms 94:22

Yahwe amekuwa mnara wangu wa juu

Hapa "mnara" ni sitiari ya ulinzi. "Yahwe amenilinda dhidi ya adui zangu"

Mungu amekuwa mwamba wangu na ngome yangu

Mwandishi anazungumzia Mungu kumlinda kana kwamba Mungu ni sehemu ambayo mwandishi wa zaburi anaweza kwenda ili kuwa salama. "Nimemwomba Mungu kunilinda, na ameniweka salama kwa uwezo wake"

Atawaletea juu yao udhalimu wao wenyewe

Maana zinazowezekana ni 1) "Atawafanyia vitu viovu walivyowafanyia wengine" au 2) "Atawaadhibu kwa matendo maovu yote aliyowatendea wengine."

atawakata

Hii ni lahaja inayomaanisha "atawaua"

katika uovu wao wenyewe

Maana zinazowezekana ni 1) "wakati wanafanya mambo maovu" au 2) "kwa sababu wamefanya mambo maovu."

Psalms 95

Psalms 95:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

mwamba wa wokovu wangu

Mwandishi anamzungumzia Yahwe kana kwamba ni mlima ambao watu wanaweza kupanda ili wawe salama. "mwamba ambao tunaweza kwenda na Mungu atatuokoa."

tuingie katika uwepo wake

Mwandishi anazungumza kana kwamba anawaambia wasomaji kwenda katika chumba cha enzi cha mfalme. "nenda mahali alipo"

kwa shukrani

"kwa kumshukuru tunapoingia katika uwepo wake"

mkuu kwa miungu yote

Maana zinazowezekana ni kwamba Yahwe ni mfalme mkuu 1) "ambaye anatawala juu ya miungu wengine yote," au 2) "ambaye ni bora zaidi ya miungu wengine yote."

Psalms 95:4

Katika mikono yake

Hii ni lahaja inayomaanisha "katika miliki yake" au "anawajibika kwa ajili ya."

vina

sehemu za vina virefu

vinara

sehemu za juu

mikono yake iliunda

Neno "mijono" ni njia nyingine ya kusema Yahwe mwenyewe. "yeye mwenyewe aliunda"

Psalms 95:6

tupige magoti

kuweka magoti yote ardhini, mara nyingi kuonesha unyenyekevu

watu wa malisho yake

Neno "malisho" ni njia nyingine ya kusema chakula ambacho watu wanakula katika malisho, ambayo pia inamaanisha kila kitu ambacho yahwe anatoa kwa ajili ya watu wake. "sisi ni watu ambaye huwa anatupa mahitaji yetu"

malisho

eneo ambalo wanyama hupata nyasi za kula

kondoo wa mkono wake

Neno "mkono" hapa linamaanisha jinsi Yahwe anavyowalinda watu wake kama mchungaji anavyowalinda kondoo wake. "watu ambao anawalinda kama mchungaji anavyowalinda kondoo wake"

Leo—o, kwamba usikie sauti yake!

"O, kwamba usikie sauti yake leo!" Mwandishi anajiingilia makusudi katika kile alichokuwa akikisema.

utasikia sauti yake

Hapa "sauti yake" inamaanisha kusikiliza kwa makini neno la Mungu. "msikilize kwa makini"

Psalms 95:8

Taarifa ya Jumla:

Sasa mwandishi anaandika maneno ambayo Yahwe alizungumza.

Usikaze moyo wako

"Usiwe msumbufu"

Meriba, ... Masa

Haya ni maeneo jangwani ambayo Musa aliyataja kwa sababu Waisraeli waliasi dhidi ya Mungu.

walinijaribu ... kunipima

Misemo hii miwili yote ni sitiari ya watu kuangalia ni kiasi gani cha uovu wanaweza kufanya kabla Mungu hajawaadhibu. Misemo hii inasema kitu kimoja na inaweza kuunganishwa. "walinijaribu" au "walitaka kuona kama wanaweza kufanya uovu bila ya adhabu yangu ... walinipima kama nitaendelea kuwa mvumilivu nao"

matendo yangu

"vitu vya ajabu nilivyofanya"

Psalms 95:10

Taarifa ya Jumla:

Yahwe anaendelea kuzungumza moja kwa moja na watu wake.

miaka arobaini

"miaka 40"

kizazi hicho

"watu hao wote" au "kizazi hicho chote cha watu"

zurura pembeni

Mungu anawazungumzia watu kana kwamba ni kondoo ambao wataenda popote wanapotaka na hawatabaki karibu na mchungaji. "sogea mbali na mimi" au "kwenda njia yao wenyewe"

hawajajua njia zangu

"hawajanitii"

njia zangu

"jinsi ninavyotaka waishi"

sehemu yangu ya kupumzika

"sehemu ambayo ningewaruhusu wapumzike'

Psalms 96

Psalms 96:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

wimbo mpya

wimbo ambao hakuna mtu aliyewahi kuimba

dunia yote

Hii inamaanisha watu wa duniani. "nyie watu wote mnaoishi duniani"

barikini jina lake

neno "jina" linamaanisha Yahwe mwenyewe. "mbarikini Yahwe" au "fanya kinachomfanya Yahwe afurahi."

tangazeni wokovu wake

"tangazeni kwamba ametuokoa" au "waambie watu kuwa yeye ndiye aokoae"

Psalms 96:3

Tangazeni utukufu wake katika mataifa

"Waambie watu katika kila taifa kuhusu utukufu wake mkuu"

Yahwe ni mkuu na ni wakusifiwa sana

"Yahwe ni mkuu. Msifuni sana" au "Yahwe ni mkuu, na watu wanapaswa kumsifu sana"

Yeye ni wa kuogopwa zaidi ya miungu mingine yote

"Mcheni zaidi ya miungu mingine yote"

Psalms 96:5

katika uwepo wake

"ambapo alipo"

Uzuri na fahari ziko katika uwepo wako

Mwandishi anazungumza kana kwamba uzuri na fahari ni watu wanaoweza kusimama mbele ya mfalme. "Kila mtu anajua kuhusu uzuri wake na fahari"

Nguvu na uzuri ziko katika mahali pake patakatifu

Maneno "nguvu" na "uzuri" ni njia nyingine ya kusema agano la sanduku la amri, ambayo ipo katika mahali patakatifu. "Ni mahali pake patakatifu ambapo kuna sanduku la agano la amri"

Psalms 96:7

Mpeni Yahwe sifa ... mpeni Yahwe kwa utukufu wake na nguvu

"Msifuni Yahwe ... msifuni Yahwe kwa kuwa anautukufu na nguvu."

Mpeni Yahwe utukufu ambao jina lake linastahili

"Mpeni heshima Yahwe kama jina lake linavyostahili" au "Tangaza kuwa Yahwe ni mtukufu kama jina lake linavyostahili."

jina lake

"jina" linamaanisha Mungu. "yeye"

nyua zake

baraza la hekalu ambapo makuhani walitoa sadaka ya wanyama kwa Yahwe

Psalms 96:9

Yahwe mkiwa mmevaa mavazi yanayotukuza utakatifu wake

Mtu anapaswa kuvaa mavazi yanayoonesha kuwa anelewa kwamba Yahwe ni mtakatifu. "Yahwe, na vaeni nguo za kufaa kwa sababu yeye ni mtakatifu."

Tetemekeni

kutetemeka kwa sabau ya hofu

dunia yote

"watu wote wa duniani"

Dunia pia imethibitishwa

Alithibitisha pia dunia"

haiwezi kutikiswa

"hakuna kitu kinachoweza kuitikisa"

Psalms 96:11

Acha mbingu zifurahi, na dunia ishangilie

Maana zinazowezekana ni 1) mwandishi wa zaburi anazungumza kana kwamba "mbingu" na "dunia" zina hisia kama watu. "Acha iwe kana kwamba mbingu zimefurahi na dunia kushangilia" au 2) "Acha wale wanaoishi mbinguni wafurahi na wale wanaoishi duniani washangilie"

acha bahari liungurume na kile kinacholijaza kipige kelele ya furaha

"acha sauti iwe kama watu wengi wanamsifu Yahwe, na acha iwe kana kwamba wale wanaoishi baharini na kupiga kelele kwa furaha"

Acha mashamba yashangilie na vyote vilivyomo

"Acha mashamba na vyote vilivyomo vishangilie." Mwandishi anazungumza kana kwamba "mashamba" na wanyama wanaoishi humo wana hisia kama watu. "Acha iwe kana kwamba mashamba yenyewe na wanyama wote wanaoishi humo washangilie"

Kisha acha miti yote msituni ipige kelele

"Kisha miti yote msituni zitapiga kelele"

Anakuja kuhukumu dunia. Atahukumu dunia ... na watu

Misemo hii mitatu ina maana za kufanana; misemo miwili ya mwisho inatumika kuimarisha ule wa kwanza.

kuhukumu ... atahukumu

Maana nyingine inayowezekana ni "kutawala ... atatawala"

Ataihukumu dunia kwa haki yake

Hapa "dunia" inamaanisha watu wa duniani. "Atawahukumu watu wote wa dunia kwa haki."

watu kwa uaminifu wake

"atawahukumu watu kwa uaminifu wake"

kwa uaminifu wake

Maana zinazowezekana ni 1) "kwa usawa, kulingana na kile anachojua kuwa kweli" au 2) "kutumia kigezo kile kile kwa watu wote."

Psalms 97

Psalms 97:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

acha dunia ishangilie; acha fukwe nyingi zifurahi

Dunia na fukwe zinasemwa kuwa na hisia kama watu. "Shangilieni muwe na furaha kila mtu duniani na karibu na bahari"

fukwe

Maana zinazowezekana ni 1) "nchi karibu na bahari" au 2) "visiwa."

Mawingu na giza vinamzunguka

"Hatuwezi kumwona; ni kana kwamba alikuwa amekaa gizani na mawingu yamemzunguka"

Haki na hukumu ni msingi wa kiti chake cha enzi

Neno "kiti cha enzi" ni njia nyingine ya kusema matendo na maneno ya yule anayeketi hapo. Mwandishi wa zaburi anazungumza kana kwamba haki na hukumu ni vitu halisi vilivyopafanya kiti cha enzi kuwa imara. "Yeye ana haki katika kila kitu anachofanya" au "Anaweza kutawala kwa sababu anatawala kwa haki"

msingi wa kiti chake cha enzi

Hapa "msingi wa kiti chake cha enzi" unamaanisha jinsi Yahwe anavyotawala ufalme wake.

Psalms 97:3

Moto huenda mbele yake

Mwandishi wa zaburi anazungumza kana kwamba alikuwa ni mtu anayetembea mbele ya mfalme Yahwe na kuwaambia watu kuwa mfalme anakuja.

kuwameza adui zake

"anawaunguza adui zake"

dunia huona na kutetemeka

"dunia" inamaanisha watu wanaoishi duniani. "watu wa duniani wanaona na kutetemeka"

kutetemeka

"anatetemeka kwa uoga"

Milima inayeyuka kama nta mbele ya Yahwe

"Milima haiwezi kusimama wakati Yahwe anakuja karibu" au "Milima inaporomoka katika uwepo wa Yahwe"

Psalms 97:6

Anga zinatangaza haki yake

Maana zinazowezekana ni 1) mwandishi wa zaburi anazungumza kana kwamba anga ni wajumbe wa Yahwe wanaotangaza kuwa Yahwe ni wa haki. "Kila mtu anaweza kuona kuwa Mungu ni wa haki, kwa njia ilie ile ambayo wote wanaliona anga" au 2) anga inamaanisha viumbe vinavyoishi mbinguni. "Wale wote wanaoishi mbinguni wanatangaza kwamba Yahwe ni wa haki"

Wale wote wanaoabudu sanamu za kuchonga wataaibika, wale wanaojivunia katika sanamu zisizofaa

"Mungu atawaaibisha wale wote wanaojivunia katika sanamu zisizofaa na kuabudu sanamu za kuchonga"

Sayuni ikasikia ... miji ya Yuda

Hii inamaanisha watu wanaoishi katika nchi hizi. "Watu wa Sayuni walisikia ... watu wa Yuda"

Psalms 97:9

uko juu zaidi ya dunia yote

Mwandishi wa zaburi anazungumza kana kwamba wale wenye nguvu ya kutosha ya kutawala walikuwa juu zaidi kimwili zaidi ya wengine. "unatawala juu ya watu wote wanaoishi"

Umetukuzwajuu zaidi

Mwandishi anazungumza kana kwamba wale wenye nguvu ya kutosha ya kutawala walikuwa juu zaidi kimwili zaidi ya wengine. "Uko juu, mbali"

mkono wa mwovu

"nguvu ya waovu"

Nuru imepandwa kwa ajili ... na furaha kwa ajili ya

Misemo hii miwili ina maana za kufanana na inatumika pamoja kwa ajili ya kuweka mkazo. "Yahwe anapanda nuru kwa wale wanaofanya ya haki, na anapanda furaha kwa ajili ya wale wenye unyoofu wa mioyo"

Nuru imepandwa kwa ajili ya wenye haki

Neno "kupanda" ni sitiari ya matendo yenye matokeo ya mbeleni. "Nuru" ni sitiari ya vitu vizuri. "Yahwe anapanga vitu vizuri viwatokee watu wenye haki mbeleni"

wenye haki

"watu wenye haki"

na furaha kwa wale wenye mioyo ya uaminifu

"na furaha inapandwa kwa ajili ya wale wenye unyoofu wa mioyo." Neno "kupanda" ni sitiari ya matendo yenye matokeo ya mbeleni. "Yahwe anapanga kwa ajili ya watu wake wenye unyoofu wa mioyo kuwa na furaha siku za mbele"

wale wenye mioyo ya uaminifu

Moyo unamaanisha mtu mzima. "mtu mnyoofu"

Psalms 97:12

Taarifa ya Jumla:

Mstari huu una amri unaofuatwa na sababu ya amri hiyo. "Kwa sababu ya kile ambacho Yahwe amewafanyia, nyie watu wenye haki, kuweni na furaha na mpeni shukrani mnapokumbuka utakatifu wake"

Furahini katika Yahwe

"Furahini kwa sababu ya kile ambacho Yahwe amewatendea"

mnapokumbuka utakatifu wake

Maana zinazowezekana ni 1) "mnapokumbuka jinsi alivyo mtakatifu" au 2) "kwa jina lake tukufu," ni njia nyingine ya kusema "kwake."

Psalms 98

Psalms 98:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

wimbo mpya

wimbo ambao hakuna mtu amewahi kuimba.

mkono wake wa kuume na mkono wake mtakatifu umempa

Maneno "mkono wake wa kuume" na "mkono wake mtakatifu" zinamaanisha nguvu ya Yahwe. Pamoja zinasisitiza ukuu wa nguvu yake ulivyo. "uwezo wake mkuu sana umempa"

mkono wake wa kuume

mkono wenye nguvu na ujuzi zaidi

mkono wake mtakatifu

Hapa "mkono" ni sitiari ya uwezo. "uwezo ulio wake pekee"

umempa ushindi

Maana zinazowezekana ni 1) "kumwezesha kuwashinda adui zake" au 2) "kumwezesha kuwaokoa watu wake"

amefanya wokovu wake kujulikana

Nomini dhahania "wokovu" inaweza kutafsiriwa kwa kutumia kitenzi "oka." "amewaonesha watu kuwa huokoa watu wake"

ameonesha haki yake kwa mataifa yote

Neno "mataifa" ni njia nyingine ya kusema watu wanaoishi katika mataifa yote. "amewaonesha watu wanaoishi katika mataifa yote kuwa yeye ni wa haki"

Psalms 98:3

Anaitisha akilini

"anakumbuka"

mwisho wote wa dunia ... dunia yote

Hizi ni njia zingine za kusema watu wa duniani. "watu kutoka duniani kote .. watu wote duniani"

wataona utukufu wa Mungu wetu

Nomino dhahania inaweza kutafsiriwa na kitenzi "kushinda." "watamwona Mungu wetu akiwashinda adui zake"

pasukeni katika wimbo

"kuanza kuimba ghafla kwa furaha"

imbeni kwa furaha

"imbeni kwa sababu mnafuraha"

imbeni sifa

"imbeni sifa kwa Mungu"

Psalms 98:5

tuni

sauti nzuri ya muziki ya kupendeza

baragumu

pembe la mnyama linalotumika kama chombo cha muziki

fanyeni kelele ya shangwe

"inueni shangwe"

Psalms 98:7

Acha bahari ipige kelele na kila kitu kilichomo

Mwandishi wa zaburi anazungumza kana kwamba bahari ni mtu anayeweza kupaza sauti kwa Mungu. "Iwe kana kwamba bahari na kila kitu kilichomo kinapiga kelele"

dunia na wote wanaoishi ndani yake

Mwandishi wa zaburi anazungumzia dunia kana kwamba ni mtu. "na acha dunia na wote wanaoishi ndani yake wapige kelele"

Acha mito ipige makofi, na milima ipige kelele ya shangwe

Mwandishi anazungumza kana kwamba mito na milima ni watu wanaoweza kupiga makofi na kupiga kelele. "Iwe kana kwamba mito inapiga makofi na milima inapiga kelele ya furaha"

dunia ... mataifa

Misemo hii ni njia nyingine ya kusema "watu wa duniani" na "watu wanaoishi katika mataifa"

mataifa kwa usawa

"atahukumu mataifa kwa usawa"

kwa usawa

"ukweli" au "kutumia kigezo sawa kwa kila mmoja"

Psalms 99

Psalms 99:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

mataifa

Hii inamaanisha watu wa mataifa. "watu wa mataifa yote"

yatetemeke

kutetemeka kwa hofu

Ameketi amesimikwa juu ya makerubi

Mwandishi wa zaburi anazungumza kana kwamba kiti cha enzi ambacho yahwe hukaa ni juu ya makerubi kwenye mfuniko wa amri za sanduku la agano hekaluni.

inatetemeka

inatikisika

Yahwe ni mkuu Sayuni; ameinuliwa juu ya mataifa yote

"Sio tu kwamba Yahwe ni mkuu sayuni, ametukuka juu ya mataifa yote" au "Sio tu kwamba Yahwe anatawala Sayuni, anatawala juu ya mataifa yote"

ameinuliwa juu ya mataifa yote

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "watu katika mataifa yote wanamtukuza" au "watu katika mataifa yote wanamsifu sana"

Acha walisifu jina lako kuu na la ajabu

Hapa mwandishi anahama kutoka kumzungumzia Mungu na kuzungumza na Mungu. Ingawa baada ya msemo huu, anarudi tena kumzungumzia Mungu.

Psalms 99:4

anapenda haki

Nomino dhahania "haki" inaweza kutafsiriwa kutumia msemo "kilicho cha haki." "anapenda kufanya kilicho cha haki"

Umeimarisha usawa

Nomino dhahania ya "usawa" ni njia nyingine ya kusema sheria zilizo na usawa. "Sheria ulizoweka zina usawa"

miguuni pake

"mbele ya kiti chake cha enzi"

Psalms 99:6

dhabiti

"takatifu"

Psalms 99:8

Ukawajibu

"ukawajibu watu wako"

kilima chake kitakatifu

"Mlima Sayuni"

Psalms 100

Psalms 100:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Piga kelele ya furaha kwa Yahwe

"Paza kelele kwa Yahwe."

dunia yote

Hii inamaanisha watu tote wa duniani. "kila mtu duniani"

njooni mbele zake

Mwandishi wa zaburi hii anazungumza kana kwamba anawaambia watu kwenda kwenye chumba chenye kiti cha enzi cha mfalme. "nenda mahali alipo kwa kuimba kwa furaha" au "anaweza kukusikia, kwa hiyo imba kwa furaha"

Psalms 100:3

kondoo wa malisho yake

Watu wa Mungu ni kama kondoo. "watu ambao Mungu anawahudumia na kuwalinda"

malisho

sehemu yenye nyasi ya kulishia wanyama

Psalms 100:4

na shukrani

"wakati ukimshukuru" au "huku ukimpa shukrani"

barikini jina lake

Neno "jina" ni njia nyingine ya kusema Yahwe mwenyewe. "mbariki Yahwe" au "fanya yale yatakayo mfurahisha Yahwe."

ukweli wake katika vizazi vyote

"ukweli wake unadumu katika vizazi vyote"

katika vizazi vyote

"kizazi baada ya kizazi."

Psalms 101

Psalms 101:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Psalms 101:2

Nitatembea katika njia ya uaminifu

Hapa Daudi anazungumza kuhusu "kuishi" kana kwamba ni "kutembea." "Nitaishi kwa namna ambayo ni ya uaminifu na sawa" au "Nitaishi maisha yaliyo jaa uaminifu"

Nitatembea na uaminifu ndani ya nyumba yangu

Hapa Daudi anazungumza kuhusu "kuishi" kana kwamba ni "kutembea." Pia, Daudi anazungumzia kuhusu kuangalia nyumba yake kwa uaminifu , kana kwamba uaminifu ni kitu cha kimwili kinachokaa ndani ya nyumba yake. "Nitaichunga nyumba yangu kwa uaminifu"

Sitaweka uovu mbele ya macho yangu

"Uovu" ni nomino dhahania inayoweza kuandikwa kama msemo. Lahaja, "weka uovu mbele ya macho yangu," inamaanisha kuukubali. "Sitakubali mtu kufanya kisicho sawa mbele yangu"

haitang'ang'ania kwangu

Daudi anaelezea "uovu" kana kwamba ni kitu kinachoweza kumng'ang'ania. Hii inamaanisha ataepuka vitu viovu na watu wanaofanya vitu viovu. "Nitajiepusha kabisa na uovu"

ng'ang'ania

kushikilia kitu au mtu kwa nguvu.

Psalms 101:4

uovu

"chochote kilicho kiovu"

mwenye mwenendo wa dharau na kiburi

Misemo hii miwili ina maana moja na inasisitiza jinsi watu wa hivyo walivyo na kiburi.

mwenendo

"fikra" au "tabia"

Nitamtazama mwaminifu wa nchi kuketi pembeni kwangu

Hii inamaanisha kuwa Daudi angewaruhusu wale watu hao kuwa karibu naye na kuishi naye. "Nitawaruhusu waaminifu wa nchi kuishi na mimi"

mwaminifu

Hii inamaanisha watu walio waaminifu kwa Mungu. "watu waaminifu"

wanaotembea katika njia ya uadilifu

Hapa Daudi anazungumzia "kuishi" kana kwamba ilikuwa "kutembea." "ishi kwatika njia iliyo ya uwazi na sawa" au "wanaoishi maisha yaliyojaa uadilifu"

Psalms 101:7

Watu waongo hawata ... waongo hawata..

Misemo hii miwili ina wazo moja na inatumika pamoja kusisitiza jinsi Daudi atakavyoshindwa kuwavumilia watu waongo.

waongo hawatakaribishwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Sitawakaribisha waongo"

mbele ya macho yangu

Hapa "macho yangu" yanaashiria Daudi mwenyewe. "mbele yangu" au "mbele ya uwepo wangu"

Asubuhi kwa asubuhi

"Kila siku"

waovu

Hii inamaanisha watu waovu. "watu waovu"

kutoka mji wa Yahwe

Daudi anamaanisha mji aliumo kama "mji wa Yahwe." Hii inaweza kuwekwa wazi. "kutoka kwenye mji, ambao ni mji wa Yahwe"

Psalms 102

Psalms 102:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

aliyeteswa

Hii inamaanisha mtu aliyeteswa. "mtu aliyeteswa"

anapolemewa

"dhaifu" au "mnyonge"

kumwaga maombolezo yake mbele ya Yahwe

Jinsi mtu anavyoeleza maombolezo yake inafananishwa na kumwaga kimiminiko. "anaeleza huzuni yake kwa uhuru kwa Yahwe"

Psalms 102:3

siku zangu zinapita kama moshi

Hapa "siku zangu" inamaanisha maisha ya mwandishi na wazo la "moshi" ni kitu kinachopotea upesi. "maisha yangu yanapita upesi"

mifupa yangu kama moto

Hapa mwandishi anazungumzia "mwili" wake kama "mifupa." "nahisi mwili wangu ni kama kitu kinachoungua"

Moyo wangu umepondeka

Hapa mwandishi anajizungumzia mwenyewe kama "moyo"wake. "Niko katika huzuni"

niko kama nyasi ziizonyauka

Hii ni njia nyingine ya kuelezea huzuni yake. "nahisi kama vile nakauka kama nyasi zilizonyauka"

Psalms 102:5

Nimekuwa kama mwari wa jangwani

Analinganisha upweke wake na ule wa mwari, ambayo mara nyingi huonekana yenyewe badala ya kuwa ndege wengine. "Nimekuwa mpweke na niliyechukiwa kama mwari jangwani"

mwari

ndege mkubwa anaye kula samaki

nimekuwa kama bundi katika maanguko

Mwandishi anaendelea kufafanua upweke kwa kujifananisha mwenyewe na bundi katika maanguko yaliyotelekezwa. "nimekuwa mwenyewe kama bundi katika maanguko yaliyo telekezwa"

bundi

Huyu ni ndege anayekuwa macho wakati wa usiku. "ndege wa usiku"

Psalms 102:7

Ninalala macho kama ndege mpweke

Mwandishi anajifananisha na ndege kusisitiza hisia yake ya upweke.

Psalms 102:9

Ninakula majivu kama mkate

Daudi angekuwa amekaa katika majivu kama kitendo cha kuomboleza, kwa hiyo majivu yangeanguka kwenye chakula chake. "Ninakula majivu kama ninavyokula mkate" au "Ninapoomboleza, majivu hudondoka kwenye mkate ninaokula"

na kuchanganya kinywaji changu na machozi

Daudi hakuchanganya kwa makusudi kinyaji chake na machozi; bali chozi lake lingedondoka katika kikombe chake wakati akiomboleza na kulia. "na machozi yangu yanadondoka kwenye kikombe ninachonywea"

umeniinua juu kunitupa chini

Mungu hajainua kiuhalisia mwili wa Daudi na kuutupa ardhini; bali Daudi anasema hivi kuelezea anachojisikia na kupitia. "ni kana kwamba umeniinua juu ili kunitupa chini"

Psalms 102:11

Siku zangu ni kama kivuli kinachofifia

Daudi anafananisha muda aliobakiza kuishi duniani na kivuli kinachofifia. "Muda wangu wa kubaki hai ni mfupi kama kivuli cha jioni ambacho kitapotea punde"

nimenyauka kama nyasi

Wakati mwili wa Daudi unakuwa mdhaifu na anakaribia mwisho wa maisha yake, anajilinganisha na nyasi zinazonyauka. "mwili wangu umedhofika kama nyasi zilizonyauka"

nyauka

kukauka na kujikunja

umaarufu wako ni wa vizazi vyote

"utatambulika katika vizazi vyote vitakavyokuja"

umaarufu

kujulikana na watu wengi

Psalms 102:13

kuwa na huruma juu ya Sayuni

Hapa "Sayuni" inamaanisha watu wanaoishi Sayuni. "kuwa na huruma na watu wanaoishi Sayuni"

juu yake

Neno "yake" inamaanisha Sayuni.

hushika mawe yake karibu

"Mawe" inamaanisha mawe yaliyokuwa sehemu wa kuta za mji kabla ya kuangamizwa. "bado wanapenda mawe yaliyokuwepo katika kuta za mji"

jina lako

Hapa "jina lako" linamaanisha Yahwe. "wewe"

wataheshimu utukufu wako

Watu watumheshimu Yahwe kwa sababu ya utukufu wake. Hapa Yahwe anazungumziwa kwa utukufu wake. "watakuheshimu wewe kwa sababu una utukufu"

atatokea katika utukufu wake

"ataonekana kama mtukufu" au "watu wataona utukufu wake"

Psalms 102:17

fukara

Hii inamaanisha watu fukara.

hatakataa maombi yao

"Yahwe atakubali maombi yao"

Hii itaandikwa kwa ajili ya vizazi vya baadaye

"Nitaandika hii kwa ajili ya vizazi vya baadaye"

Psalms 102:19

Kwa kuwa ametazama chini kutoka katika patakatifu pake pa juu; kutoka mbinguni Yahwe ametazama

Misemo hii miwili ina maana za kufanana na inatumika pamoja kusisitiza jinsi Mungu anavyotazama chini kutoka mbinguni.

patakatifu pake pa juu

"mahali pake patakatifu juu ya dunia"

wale walio hukumiwa kufa

"wale ambao mamlaka yaliwaamuru kuhukumiwa kufa"

Psalms 102:21

tangaza jina la Yahwe katika Sayuni na sifa zake katika Yerusalemu

Misemo hii miwili inamaana moja na inasisitiza wazo la kusifu jina la Yahwe.

na sifa zake

"na tangazeni sifa zake"

Psalms 102:23

amechukuwa nguvu yangu

Daudi anazungumzia Mungu kumsababisha kuwa mnyonge kana kwamba nguvu yake ni kitu cha kihalisia kinachoweza kuondolewa kutoka kwake. "amenisababisha kuwa mnyonge"

siku zangu

Neno "siku" hapa linamaanisha maisha. "maisha yangu"

usichukue

Daudi anamwomba Mung asimwache afe. "usinitoe kutoka duniani" au "usiniache nife"

upo hapa katika vizazi vyote

"uko katika vizazi vyote"

Psalms 102:25

wote watazeeka

Neno "wote" linamaanisha "dunia" na "mbingu."

miaka yako haitakuwa na mwisho

Hapa Daudi anaelezea urefu wa muda ambao Mungu yuko hai kama "miaka" yake. "utaishi milele"

Psalms 102:28

wataishi

"wataendelea kuishi"

wataishi katika uwepo wako

Hapa Daudi anaelezea uzao kulindwa na Yahwe kama kuwa katika uwepo wake. "watalindwa wanapoishi katika uwepo wako"

Psalms 103

Psalms 103:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Nitamsifu Yahwe na maisha yangu yote, na kwa vyote vilivyo ndani yangu, ninatoa sifa kwa jina lake takatifu, ninatoa sifa kwa jina lake takatifu

Misemo hii miwili inamaana moja na inasisitiza jinsi atakavyomsifu Yahwe. "Nitamsifu Yahwe kwa moyo wangu wote"

ninatoa sifa kwa jina lake takatifu

Hii inamaanisha kusifu jina la Yahwe kama Yahwe.

vyote vilivyo ndani yangu

"kila kitu ndani yangu." Daudi anatumia msemo huu kujizungumzia mwenyewe na kusisitiza mapenzi kwa Yahwe.

Psalms 103:3

zako ... yako

Tafsiri nyingi zinaeleza hii na "mimi."

Anakomboa maisha yako kutoka katika uharibifu

Hii inamaanisha kuwa Yahwe anamweka kuwa hai. "Ananiokoa kutoka na kifo"

anakuvika taji

Hapa "baraka' inaelezwa kana kwamba ni "kuvikw taji." "anakubariki"

Anakuridhisha maisha yako na vitu vizuri

Msemo "maisha yako" inamaanisha "wewe," lakini inasisitiza kuwa Yahwe hutoa baraka katika maisha yote. "Anakuridhisha na vitu vizuri katika maisha"

ujana wako unafanywa kuwa mpya kama tai

Kuwa na "ujana wako kufanywa kuwa mpya" inamaanisha kujihisi kijana tena. Hapa Daudi anafananisha hisia hii ya ujana na wepesi na nguvu ya tai. "unajihisi kijana na mwenye nguvu kama tai"

ujana wako

"ujana" unamaanisha nguvu ambayo alikuwa nayo kama kijana.

Psalms 103:6

anafanya vitendo vya hukumu kwa ajili ya

"anasababisha hukumu kutokea"

wote walio kandamizwa

"wote walio kandamizwa na watu"

matendo yake kwa uzao

"alifanya matendo yake yajulikane kwa uzao"

ana uaminifu mkuu wa agano

amejaa huruma na upendo"

Psalms 103:9

Hataadabisha wakati wote; hakasiriki kila mara

Misemo hii miwili ina maana za kufanana. Msemo wa pili unaimarisha wazo la kwanza.

Hatufanyii ... au kutulipa

Misemo hii miwili ina usambamba na inasisitiza kwamba Mungu hatuadhibu kama tunavyostahili. "Hatulipi kwa adhabu tunayostahili kwa ajili ya dhambi zetu"

Hatufanyii

"Hautuadhibu"

Psalms 103:11

Kwa kuwa kama anga zilivyo juu ... kuelekea wale ambao humheshimu

Tashbihi inalinganisha umbali mkubwa kati ya mbingu na dunia kwa ukuu wa upendo wa Mungu kwa ajili ya watu wake.

Kama vile mashariki ilivyo mbali ... alivyoondoa hatia ya dhambi zetu kutoka kwetu

Umbali kati ya mashariki na magharibi ni mbali sana mpaka haiwezi kupimika. Katika tashbihi hii, umbali huo unalinganishwa kwa jinsi Mungu anavyosogeza mbali hatia yetu kutoka kwetu.

Kama vile baba alivyo na huruma ... juu ya wale amabo humheshimu

Hapa mwandishi analinganisha huruma ya baba kwa watoto wake kwa huruma ya Yahwe kwa wale ambao wanamheshimu.

Psalms 103:14

jinsi tulivyoumbwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "jinsi miili yetu ilivyo" au "jinsi alivyoumba miili yetu"

anajua ya kuwa sisi ni vumbi

Yahwe alipomuumba Adamu mtu wa kwanza alimuumba kutoka na vumbi. "anakumbuka ya kwamba alituumba kutoka na vumbi"

Na kwa mtu, siku zake ni kama nyasi

Katika tashbihi hii, urefu wa maisha ya mtu unalinganishwa na urefu mfupi ambao nyasi huota kabla hazijafa. "Urfeu wa maisha ya mtu ni kama yale ya nyasi"

hustawi kama ua katika shamba

Katika tashbihi hii, jinsi mtu hukua katika muda inalinganishwa kwa jinsi ua huota.

hustawi

"Kustawi" ni kuota vizuri na kuwa na afya.

Upepo huvuma juu yake, na linatoweka ... ni wapi liliwahi kuota

Misemo hii inaendelea kuongea juu ya maua na nyasi. Inalinganisha jinsi maua na nyasi hufa kwa jinsi mtu hufa. "Upepo huvuma juu ya maua na nyasi na inapotea, na hakuna awezaye kujua wapi zilianza kuota - ni sawa na mwanadamu"

Psalms 103:17

ni kutoka milele mpaka milele

Hii ina maana ya kwamba upendo wa Yahwe huendelea milele. "utaendelea milele"

vizazi vyao

"vizazi vya wale ambao humuinua yeye"

Wanashika agano lake na kukumbuka kutii maelekezo yake

Misemo hii miwili ina maana za kufanana.

Yahwe ameimarisha kiti chake cha enzi katika mbingu

Hapa utawala wa Yahwe kama mfalme unamaanishwa kama "kiti chake cha enzi". "Yahwe amechukua kiti chake katika mbingu ambapo hutawala kama mfalme"

ameimarisha

"alifanya"

ufalme wake hutawala

Hapa Yahwe anaelezwa kuwa "ufalme wake" kusisitiza mamlaka yake kama mfalme. "hutawala"

Psalms 103:20

hutekeleza mapenzi yake

Hii ni lahaja ikimaanisha "kufanya mapenzi yake". "fanya mapenzi yake"

katika sehemu zote ambazo hutawala

"msifu yeye katika sehemu zote ambapo hutawala"

kwa maisha yangu yote

"na moyo wangu wote" au "na nafsi yangu yote". Msemo huu una maana ya kwamba atamsifu Yahwe kwa moyo wote na unatumika kusisitiza utii wake kwake.

Psalms 104

Psalms 104:1

Taarifa ya Jumla

Usambaba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Taarifa ya Jumla

Zaburi hii ni wimbo wa sifa.

kwa maisha yangu yote

"kwa moyo wangu wote" au "kwa nafsi yangu yote". Msemo huu una maana ya kwamba atamsifu Yahwe kwa moyo wote na inatumika kusisitiza utii wake kwake.

umevaa ufahari na utukufu

Maneno "ufahari" na "utukufu" ina maana moja na inasisitiza ukuu wa utukufu wa Yahwe. Inaelezwa kama kumvisha Yahwe kama vazi. "una ufahari na utukufu kukuzunguka kote"

Unajifunika kwa mwanga kama vile vazi

Yahwe anafafanuliwa kama kufunikwa na mwanga kana kwamba mwanga ulikuwa vazi kukuzunguka. "Unafunikwa na mwanga"

unatandaza nje mbingu kama pazia la hema

Hapa Mungu anafafanuliwa kama kutandaza nje mbingu kama mtu anavyotandazwa nje ya hema wakati inaandaliwa. "unatandaza nje mbingu kama mtu anayetengeneza hema"

Unalaza nguzo za chumba chako juu ya mawingu

"Unajenga vyumba vyako vya juu katika mbingu". Hii ina maana ya nyumba yake kuwa ndefu ya kwamba sakafu yake ya juu inatanuka mapka katika mawingu.

unafanya mawingu kuwa kibanda wazi chako

Hapa mawingu yanaelezwa kumbeba Yahwe kana kwamba yalikuwa kibandawazi. "unafanya mawingu kukubeba kama kibandawazi"

unatembea juu ya mabawa ya upepo

Hapa kuvuma kwa upepo inaelezwa kama mabawa ambayo Yahwe hutembea. "unatembea juu ya upepo"

Psalms 104:4

Hufanya upepo kama wajumbe wake

Maana zaweza kuwa 1) anasababisha upepo kuweza kubeba ujumbe kama mjumbe, "Hufanya upepo kuwa kama wajumbe wake" au 2) "Huwafanya wajumbe wake kuwa na haraka kama upepo"

miale ya moto watumishi wake

Maana zaweza kuwa 1) "anasababisha miale ya moto kuwa kama watumishi wake". Husababisha moto kumtumikia kama mtumishi angefanya au 2) "hufanya mtumishi wake kuwa kama miale ya moto".

miale ya moto watumishi wake

Hii inaweza kuandikwa na taarifa ya kudokezwa kutoka katika mstari wa nyuma. "Hufanya miale ya moto watumishi wake"

Alilaza misingi ya dunia

Hapa msemo "kulaza misingi" ina maana ya "kuumbwa". "Aliumba dunia nzima"

Psalms 104:6

Ulifunika dunia kwa maji kama vazi

Hapa maji ambayo yalifunika dunia inalinganishwa na jinsi vazi kubwa linavyoweza kufunika kabisa kitu. "Umefunika kabisa dunia kwa maji"

Kukaripia kwako hufanya maji ... yalitoroka

Misemo hii miwili ina maana moja na inatumika pamoja kusisitiza jinsi Mungu alivyozungumza na maji yalivyoondoka.

kurudi nyuma

"kukimbia" au "kusogea nyuma"

yalitoroka

Hapa mtunga zaburi anazungumza juu ya maji kurudi nyuma kana kwamba yalitoroka kama mnyama baada ya kusikia sauti ya Yahwe. Neno "kutoroka" lina maana ya kukimbia mbali haraka. "kukimbia haraka"

Psalms 104:8

Milima ikainuka, na mabonde yakasambaa

Hapa mtunga zaburi anazungumza juu ay Mungu kusababisha milima na mabonde kusogea na kubadilika kana kwamba zilichagua kusogea zenyewe. Inaelezewa kwa njia hii kusisitiza uwezo wa Mungu.

mpaka kwa ajili yao ili wasivuke

Hapa mtunga zaburi anazungumza juu ya Mungu kusababisha maji kutovuka mpaka ambao alitengeneza kwa ajili yao kana kwamba maji yenyewe yalichagua kutovuka. Yaneelezewa kwa naman hii kusisitiza mamlaka ya Mungu juu yao. "mpaka kwa ajili yao ambao hawawezi kuvuka"

mpaka

"mstari" au "mpaka"

kwa ajili yao

Neno "yao" ina maana ya maji.

Psalms 104:10

vijito

mito midogo

punda pori huzima kiu yao

Inaweza kuwekwa wazi ya kwamba wanazima kiu yao kwa kunywa maji. "punda pori hunywa maji kuzima kiu yao"

ukingo wa mto

ardhi katika ukingo wa mto

wanaimba miongoni mwa matawi

Hapa Daudi anafafanua ndege kulia kana kwamba walikuwa wakiimba. "wanalia miongoni mwa matawi ya mti"

Psalms 104:13

Humwagilia milima kutoka katika vyumba vyake vya maji vya angani

Hii ina maana ya kwamba Mungu husababisha mvua kunyesha. Maji yanaelezwa kama kurudi nyuma katika vyumba vya angani. "Humwagilia milima kwa kusababisha mvua kuanguka kutoka angani"

matunda ya kazi yake

"mambo mengi mazuri ambayo unaumba"

na mimea kwa ajili ya mtu kulima

Maneno ambayo hayapo yanweza kuongezwa. "na hufanya mimea kuota kwa ajili ya mtu kulima"

Psalms 104:16

Miti ya Yahwe hupata mvua nyingi

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe alitoa mvua nyingi kwa ajili ya miti yake"

Pale ndege hutengeneza viota vyao

Wanatengeneza viota vyao katika seda. Hii inaweza kuwekwa wazi. "Ndege hutengeneza viota vyao katika seda"

korongo

Huyu ni aina ya ndege. "ndege"

pimbi

Pimbi ni mnyama mdogo ambaye hufanana na panya mkubwa. "melesi wa mawe"

Psalms 104:19

nyakati

Neno hili lina maana ya hali za hewa tofauti zinazobadilika katika mwaka. Baadhi ya sehemu zina nyakati za mvua kubwa na kiangazi, wakati zingine zina majira ya kuchipua, majira ya bubujiko, majira ya joto na majira ya baridi.

jua linajua wakati wake

Hapa Daudi anafafanua jua kana kwamba anajua ni wakati gani wa siku. "alifanya jua kuzama muda ukiwadia"

Unafanya

"Yahwe, unafanya". Hapa mwandishi anabadilisha kutoka kuzungumza juu ya Yahwe kwa kuzungumza kwake.

Psalms 104:21

mawindo

Huyu ni mnyama ambaye ni chakukla kwa ajili mnyama mwingine.

na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu

"lakini wanamtegemea Mungu kutoa chakula chao"

kurudi nyuma

"rudi" au "ondoka mbali"

mapango

nyumba za baadhi ya mamalia na wanyama wadogo

Psalms 104:23

humwagikia kwa kazi zako

Hapa Daudi anafafanua kiasi cha vitu ambavyo Yahwe aliviumba kana kwamba vilikuwa kimiminiko kumwagikia nje ya chombo. "inajazwa na kazi yako!"

Psalms 104:25

kirefu na kipana

"ina kina kirefu sana na ni pana sana". Urefu na upana wa bahari unasisitiza jinsi ilivyo kubwa.

inayojaa

"inayomwagikia"

visivyohesabika

"isiyohesabika"

wote wadogo na wakubwa

Hii ina maana ya viumbe vya kila aina ya ukubwa.

Meli husafiri pale

"Meli husafiri juu ya bahari"

Psalms 104:27

Hawa wote

"Viumbe hawa wote"

kuwapa chakula chao kwa wakati

"kuwapa chakula chao wanapokihitaji"

Utakapowapatia, wanakusanya

Inaweza kusaidia kuandika ya kwamba ni chakula ambacho kinapewa. "Unapotoa chakula kwao, wanakikusanya"

wanakusanya

"kusanya"

unapofungua mkono wako

Hii inaelezea Yahwe kama kufungua mkono wake kutoa chakula kwa viumbe. "unapofungua mkono wako kuwalisha"

Psalms 104:29

utakapoficha uso wako

Hii ina maana ya kwamba Yahwe hawatazami wao au kuwaangalia kwa makini. "pale ambapo hautazami juu yao" au "unapowadharau"

kurudi mavumbini

Hii ina maana ya kwamba miili yao huoza na huwa udongo tena. "miili yao huoza na kurudi ardhini"

Unapotuma nje Roho wako

Hii ina maana ya Roho wake kutumwa kutoa uhai kwa viumbe.

wanaumbwa

Ni roho ya Yahwe ambayo iliwaumba.

unafanya upya uso wa nchi

"unasababisha nchi kujaa na uhai mpya"

Psalms 104:33

mawazo yangu kuwa matamu

Analinganisha mawazo yake na kitu ambacho ni kitamu. "mawazo yangu yawe mazuri"

Psalms 104:35

wapoteleaa

"kupotelea"

acha waovu wasiwepo tena

Msemo huu "waovu" una maana ya watu waovu. "na watu waovu wapotelee"

Psalms 105

Psalms 105:1

Taarifa ya Jumla

Usambamba ni kawaida katika shairi ya Kiebrania.

liite jina lake ... Jivunie katika jina lake takatifu

Hapa "jina" inawakilisha Yahwe. "muite yeye ... Jivunie ndani ya Yahwe"

mataifa

Hii ina maana ya watu katika mataifa. "watu wa mataifa"

acha moyo wa wale ambao humtafuta Yahwe washangilie

Hapa "moyo" inawakilisha mtu ambaye humtafuta Yahwe. "acha watu ambao humtafuta Yahwe washangilie"

Psalms 105:4

Mtafute Yahwe na nguvu yake

"kutafuta nguvu ya Yahwe" ina maana ya kumuuliza kukuimarisha.

Kumbuka

"kumbuka"

miujiza yake na

Inaweza kusaidia kuongeza maneno ambayo hayapo. "kumbuka miujiza yake na"

maagizo kutoka mdomoni mwake

Hapa "mdomoni" ina maana ya mambo ambayo alizungumza. "maagizo ambayo ameyazungumza"

vizazi vyako vya Abrahamu ... nyie watu wa Yakobo

Mwandishi anazungumza kwa Waisraeli, kuwaita majina haya.

Abrahamu mtumishi wake

"Abrahamu, mtumishi wa Yahwe"

Psalms 105:7

Huweka akilini ... neno ambalo aliloliamuru

Misemo hii miwili inatumia maana ya kufanana na inatumika pamoja kwa ajili ya msisitizo. Neno "neno" lina maana ya agano. "Huweka akilini agano lako milele, ahadi aliyoifanya"

huweka akilini

Hii ina maana ya kukumbuka na kufikirir juu ya jambo. "hukumbuka"

vizazi elfu moja

"vizazi 1,000"

Psalms 105:9

Huweka akilini

Msemo huu "kuweka akilini" ina maana ya kukumbuka jambo. "anakumbuka"

agano ambalo alilifanya na Abrahamu ... kiapo chake kwa Isaka

Misemo hii miwili "agano" na "kiapo" ina maana ya ahadi moja ambayo Yahwe alifanya kwa watu wake.

kiapo chake kwa Isaka

Inaweza kusaidia kuongeza maneno ambayo hayapo. "kiapo chake ambacho alitoa kwa Isaka"

Psalms 105:12

Kauli Kiunganishi

Mtunga zaburi anaandika kuhusu Israeli.

walipokuwa wachache tu kwa idadi

Neno "walipokuwa" ina maana ya Waisraeli.

na wageni katika nchi

Inadokezwa ya kwamba "nchi" ina maana ya Kaanani. "na walikuwa wageni katika nchi ya Kaanani"

Waliondoka kutoka

"Waliendelea kutangatanga"

kutoka taifa kwa taifa na kutoka ufalme mmoja kwa mwingine

Misemo hii miwili ina maana moja na inatumika pamoja kwa msisitizo.

Psalms 105:14

Kauli Kiunganishi

Mtunga zaburi anazungumza kuhusu Israeli.

kwa ajili yao

"kwa ajili ya ustawi wao". Hii ina maana ya Israeli.

Usiwaguse watiwa mafuta wangu

Hapa "kugusa" ina maana ya kudhuru, ni kukuza ambapo Yahwe alitumia kuimarisha onyo lake kutowadhuru watu wake. "Usiwadhuru watu ambao niwewatia mafuta"

Psalms 105:16

Akaamuru njaa

"Alituma". Hii ina maana ya kwamba alisababisha njaa kutokea katika nchi.

akiba yote ya mkate

Hapa "mkate" ina maana ya chakula kwa ujumla. "akiba yote ya chakula"

Alimtuma mtu mbele yao; Yusufu

Inaweza kusaidia kuandika ya kwamba alimtuma mbele yao Misir. "Alimtuma mwanamume mbele yao Misri; alimtuma Yusufu ambaye"

Yusufu aliuzwa kama mtumishi

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Ndugu za Yusufu alimuuza kama mtumwa"

Psalms 105:18

minyororo

vizuizi vya chuma vinavyotumika kushika vifundo vya mfungwa au vifundo vya mguu pamoja

Miguu yake ilifungwa kwa minyororo; shingoni mwake kuliwekwa kola ya chuma

Kauli hizi zinaweza kuandikwa kama hali ya kutenda. "Wamisri walimfunga miguu yake kwa minyororo; waliweka kola ya chuma shingoni mwake".

neno la Yahwe likamjaribu

Hapa "neno" lina maana ya ujumbe wa Yahwe. "ujumbe wa Yahwe ulimjaribu"

Psalms 105:20

Mfalme alituma watumishi kumweka huru; mtawala wa watu akamweka huru

Misemo hii miwili ina maana moja na inatumika pamoja kwa msisitizo ya kwamba mfalme alimweka huru.

Kisha Israeli akaja mpaka Misri

Hapa "Israeli" ina maana ya Yakobo. Yakobo alileta familia yake pamoja naye. "Kisha Israeli na familia yake kuja Misri"

Psalms 105:24

Yahwe aliwafanya watu wake kuzaliana

Mwandishi anazungumza juu ya ongezeko la Israeli kana kwamba walikuwa mmea ambao ulizaa matunda mengi. "Mungu aliongeza idadi ya watu wake sana"

kuwachukia watu wake, kuwatendea vibaya watumishi wake

"kuchukia watu wake na kuwatendea vibaya watumishi wake"

Walitelekeza ishara zake ... maajabu yake katika nchi ya Hamu

Misemo hii miwili ina maana moja na inatumika pamoja kwa ajili ya msisitizo. "Musa na Haruni walitekeleza miujiza ya Yahwe Misri miongoni mwa vizazi wa Hamu"

maajabu yake

Maneno ambayo haypo yanaweza kuongezwa. "na wakatekeleza maajabu yake"

Psalms 105:28

alifanya nchi hiyo kuwa giza

"alifanya anga giza"

vyura

reptilia mdogo anayeruka

katika katika vyumba vya watawala wao

"hata walikuwa ndani ya vyumba vya watawala wao"

Psalms 105:31

Kauli Kiunganishi

Mtunga zaburi anaendelea kufafanua hukumu ya Yahwe kwa Misri.

kundi kubwa

makundi makubwa yanayopaa

chawa

wadudu wadongo wanaopaa kama nzi lakini wadogo zaidi

mvua ya mawe

barafu ambayo huanguka kutoka angani kama mvua

Aliangamiza ... alivunja

Mungu alisababisha mvua ya mawe, mvua, na radi kuharibu mizabibu na miti. "Alisababisha iangamize ... na kuvunja"

Psalms 105:34

nzige wengi sana

"kulikuwa na nzige wengi sana"

Nzige walikula mimea yote ... Walikula mazao yote ya ardhini

Misemo hii miwili ina maana moja na inatumika pamoja kwa ajili ya msisitizo. "Wadudu walikula mimea yote na mazao yote katika nchi"

Alimuua kila mzaliwa wa kwanza katika nchi, malimbuko ya nguvu zao

Hapa msemo wa pili kuhusu "malimbuko" unatumika kufafanua "mzaliwa wa kwanza" katika msemo wa kwanza. "Aliua kila mzaliwa wa kwanza katika nchi yao, ambao walikuwa malimbuko ya nguvu zao" au "Kisha Yahwe aliwaua wana wenye umri mkubwa katika kila nyumba ya watu wa Misri"

Psalms 105:37

Aliwaleta Waisraeli nje wakiwa na fedha na dhahabu

Waisraeli walipoondoka Misri walichukua fedha na dhahabu pamoja nao. "Aliwatoa Waisraeli kutoka Misri pamoja na fedha na dhahabu katika milki yao"

hakuna wa kabila lake waliojikwaa njiani

Hakuna aliyebaki nyuma. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya chanya. "makabila yake yote yaliweza kufanya safari hiyo"

Misri ilifurahi

Hapa "Misri" ina maana ya watu ambao wanaishi Misri. Watu wa Misri alifurahi.

Alitandaza wingu kuwa mfuniko

Hapa mtunga zaburi anafafanua Yahwe kuweka wingu angani kana kwamba alikuwa akitandaza nje vazi. Wingu lilikuwa "linafunika" kuwalinda kutoka na jua. "Aliweka wingu angani kuwalinda kutoka na jua na joto"

kutengeneza moto kutoa mwanga usiku

Yahwe aliweka nguzo ya moto angani kutoa mwanga wakati wa usiku. "aliweka moto angani kutoa mwanga usiku"

Psalms 105:40

naye akaleta kware

Inaweza kuwa msaada kuweka wazi ya kwamba kware ni ndege wadogo Yahwe alituma kwa ajili yao kula. "na Yahwe alituma ndege wadogo wa kula"

na mkate kutoka mbinguni

Yahwe alisababisha mana, aina ya mkate, kuanguka kutoka angani. "kwa mkate ambao ulianguka kutoka angani"

yalitiririka

"maji yalitiririka"

aliweka akilini

Hii ina maana kukumbuka. "alikumbuka"

Psalms 105:43

Akawaongoza watu wake nje ... wateule wake kwa kelele za ushindi

Misemo hii miwili ina maana moja na inatumika pamoja kusisitiza ya kwamba watu wa Mungu walikuwa na furaha alipowaongoza kutoka Misri. Watu walikuwa wakipiga kelele kwa furaha. "Aliwaongoza watu wake wateule kwa kelele za furaha na ushindi"

wateule wake

Hapa "wateule" ina maana ya watu wateule wa Yahwe. "watu wake wateule"

ushindi

"sherehe" au "furaha"

kuzishika amri zake na kutii sheria zake

Misemo hii miwili ina maana moja na inatumika pamoja kwa ajili ya msisitizo. "Kushika" amri zake ina maana ya kuzitii. "kutii sheria zake na maagizo"

Psalms 106

Psalms 106:1

Taarifa ya Jumla

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Nani awezaye kuhesabu tena matendo makuu ya Yahwe ... matendo?

Mwandishi anauliza swali hili kumsifu Mungu na hategemei jibu. "Hakuna mtu awezaye kuhesabu tena matendo makuu ya Yahwe ... matendo".

matendo yake yanayostahili sifa

"matendo ambayo yanastahili sifa"

Psalms 106:3

Niite akilini

Msemo "kuita akilini" ina maana ya kukumbuka jambo. "nikumbuke"

ya chaguo lako

Neno "aliyechaguliwa" ina maana ya watu waliochaguliwa wa Yahwe. "wa watu waliochaguliwa"

nitashangilia katika furaha ... na nitakuwa na utukufu

Haya ni mambo ambayo Daudi anasema atafanya, pamoja na "kuona mafanikio ya waliochaguliwa wako". Maneno ambayo hayaonekani yanaweza kuongezwa. "Nitashangilia katika furaha ... na nitakuwa na utukufu"

furaha

"furaha" au "shangwe"

utukufu na urithi wako

Hapa msemo "urithi wako" ina maana ya Waisraeli, ambao ni watu wa Yahwe waliochaguliwa. Hapa "utukufu" ina maana ya "kujivunia" juu ya kitu; katika hali hii wanajivunia juu ya Yahwe. "kujivunia katika ukuu wako na watu wako"

Psalms 106:6

hawakutambua mambo yako ya ajabu

"hatuna shukurani kwa ajili ya mambo ya ajabu uliyofanya"

katika bahari ... Bahari ya Matete

Misemo hii miwili ina maana ya kitu kimoja. Ya pili ni jina la bahari.

Psalms 106:8

Hata hivyo

"ingawa" au "hata hivyo"

kwa ajili ya jina lake

Hapa "jina lake" lina maana ya Yahwe. "kwa ajili ya sifa yake mwenyewe"

katikati ya vina, kama vile katikati ya nyika

Hapa Daudi analinganisha njia ambayo Yahwe aliwaongoza Waisraeli katikati ya Bahari ya Matete kwa namna watu wanaweza kuongozwa katika ardhi kavu ya nyika. "Vina" ina maana Yahwe aligawanya maji. "katikati ya Bahari ya Matiti katika ardhi kavu"

Psalms 106:10

Aliwaokoa kutoka katika mkono ... na akawaokoa kutoka katika mkono

Misemo hii miwili kimsingi ina maana moja na inatumika pamoja kusisitiza ya kwamba Yahwe aliwaokoa kutoka kwa adui zao.

mkono wa wale ambao walimchukia

Hapa "mkono" una maana ya uwezo na utawala. "uwezo wa wale ambao walimchukia" au "utawala wa wale ambao walimchukia"

yaliwafunika wapinzani wao

Hii ni njia ya upole ya kuzungumza kuhusu yao kuzama majini. "alizamisha majini maadui zake"

Kisha wakaamini maneno yake

Hapa nano "wakaamini" ina maana ya "mababu zao" na neno "yake" ina maana ya "Yahwe".

Psalms 106:13

hawakusubiri maelekezo yake

Inadokezwa ya kwamba walifanya mambo bila kusubiri kujua Yahwe alitaka waende wapi. "walifanya mambo bila kwanza kusubiri maelekezo ya Yahwe"

uchu usiotosheka

"uchu ambao hauwezi kutoshelezwa"

walishindana na Mungu

"Waliasi dhidi ya Mungu"

uliteketeza

"uliwapita" au "ulichukua"

lakini akatuma ugonjwa

Hapa Daudi anazungumza kuhusu Yahwe kusababisha watu kuumizwa kwa ugonjwa kana kwamba Yahwe alituma ugonjwa kwao kwa njia moja ambayo mtu hutuma mtu au mjumbe. "lakini alisababisha ugonjwa kuteketeza miili yao"

Psalms 106:16

Katika kambi

Hii ina maana ya kambi ya Waisraeli katika nyika. "Katika kambi nyikani"

Dunia ilifunguka na kummeza

Hapa jinsi ardhi inavyofunguka na kuwazika watu inalinganishwa kwa jinsi kiumbe kinavyomeza kitu. "Dunia ilifunguka na kuzika"

Dathani

Huyu alikuwa afisa aliyeasi thidi ya Musa.

na kuwafunika wafuasi wa Abiramu

Wafuasi wa Abiramu walizikwa pia dunia ilipofunguka na kumzika Dathani. "pia ikafunuka wafuasi wa Abiramu" au "na pia ikazika wafuasi wa Abiramu"

Abiramu

Huyu alikuwa afisa aliyeasi dhidi Musa.

Moto ukaanza miongoni mwao; moto ukawateketeza waovu

Misemo hii miwili ina maana kimoja na inaandikwa pamoja kusisitiza jinsi watu waovu waliuawa kwa moto.

Psalms 106:19

Walitengeneza ndama Horebu na kuabudu sanamu ya chuma ya kuchonga

Taarifa hii inaweza kuandikwa kwa mpangilio ili kwamba iwe wazi ya kwamba ndama alikuwa sanamu ya chuma ya kuchonga. "Horebu, walitengeneza sanamu ya chuma ya ndama na kuiabudu"

Walibadilisha utukufu wa Mungu kwa mfano wa fahali

Hii ina maana ya kwamba badala ya kumwabudu Mungu waliabudu sanamu ya fahali.

utukufu wa Mungu

Hapa Mungu anajulikana kwa utukufu wake. "Mungu wao mtukufu" au "Mungu ambaye ana utukufu"

Psalms 106:22

nchi ya Hamu

Hii ina maana ya nchi ambapo vizazi vya Hamu waliishi. "nchi ambayo uzao wa Hamu waliishi"

matendo makuu

"mambo ya ajabu"

akaingilia kati naye katika upenyu ... kutowaangamiza

Hapa Daudi anazungumzia kuhusu Musa kumshawishi Yahwe kutowaangamiza Israeli kama kuingilia kati na yeye kuwa katika upenyo. "alisimama katikati ya Yahwe na Waisraeli na kumsihi Yahwe kutowaangamiza"

Psalms 106:24

walinung'unika

"walilalamika"

ahadi yake

Hii ina maana ya ahadi ya Yahwe ya kwamba atawaruhusu kuchukua nchi ya Kaanani kama milki yao.

Psalms 106:26

akainua mkono wake

Neno "wake" ina maana ya Yahwe. Pia, ilikuwa utamaduni kuinua mkono wakati wa kutoa kiapo.

kutawanya uzao wao ... katika nchi za kigeni

Misemo hii miwili ina maana moja na inatumika pamoja kwa ajili ya msisitizo. "na ya kwamba angefanya uzao wao kuishi katika nchi za kigeni"

kutawanya

Hii ina maana ya kutawanya au kusambaza kitu

Psalms 106:28

sadaka zilizotolewa kwa wafu

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "sadaka ambazo walitoa kwa wafu"

kwa wafu

"Wafu" ina maana ya sanamu na miungu ambayo Waisraeli walikuwa wakiabudu. "Kwa miungu ambao wamekufa" au "kwa miungu ambayo haina uhai"

tauni ikazuka

"tauni ikasambaa"

Wakachochea hasira yake

"ikamkasirisha"

Psalms 106:30

Kisha Finehasi akainuka kuingilia kati

Finehasi aliingilia kati miongoni mwa watu, kuwaadhibu kwa dhambi zao. Hii inaweza kufanywa wazi. "Kisha Finehasi akainuka kuingilia kati miongoni mwa watu kwa sababu ya dhambi yao"

Ilihesabika kwake kuwa tendo la haki

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Watu walitambua lile kuwa tendo la haki"

Psalms 106:32

Meniba

Hii ni sehemu.

aliteseka kwa sababu yao

Musa aliteseka kwa sababu ya dhambi za watu. Hapa neno "yao" ni kiwakilishi nomino kwa ajili ya watu na mfano wa maneno kumaanisha dhambi yao. "aliteseka kwa sababu ya matendo yao"

lakini walichangamana na mataifa

Hapa Daudi anazungumzia watu kuoana na wanawake kutoka mataifa mengine kama "kujichanganya" pamoja nao. "lakini walijichanganya katika ndoa na mataifa mengine"

ambayo ikawa mtego kwao

Sanamu zikawa mtego kwao.

Psalms 106:37

Walimwaga damu isiyo na hatia, damu ya wana wao na binti zao

Msemo "kumwaga damu" ni tasifida inayoelezeka kutumika kwa ajili ya "mauaji". "Walimwaga damu isiyo na hatia walipowaua wana na binti zao"

Walinajisiwa kwa matendo yao

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Matendo yao yaliwachafua"

katika matendo yao wakawa kama kahaba

Hapa Daudi analinganisha kutokuwa waaminifu kwao kwa Yahwe kwa kutokuwa waaminifu kwa kahaba. "walikuwa hawana uaminifu kwa Yahwe kama kahaba"

Psalms 106:40

Kwa hiyo Yahwe alikuwa na hasira na watu wake ... akawadharau watu wake mwenyewe

"Kwa hiyo Yahwe alikuwa na hasira na watu wake na akawadharau"

Akawakabidhi katika mkono wa mataifa

Hapa "mkono" una maana ya uwezo na utawala. "Mungu aliruhusu mataifa kuwatawala"

wale waliowachukia

"watu waliowachukia"

Psalms 106:42

na wakaletwa chini ya mamlaka yao

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "na adui zao walisababisha wao kuwa chini ya mamlaka yao"

wakashushwa chini kwa dhambi yao wenyewe

Hapa msemo "kushushwa chini" ina maana ya kuangamizwa. Pia, hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "dhambi yao iliwaharibu"

Psalms 106:44

Hata hivyo

"Ingawa" au "hata hivyo".

dhiki yao

"mateso yao"

akaweka akilini

Msemo "kuweka akilini" ina maana ya kukumbuka jambo. "alikumbuka"

na akatulia

"na akawa na rehema kwao"

wanaowashinda

"waliowakamata". Hii ina maana ya maadui wa Waisraeli ambao waliwakamata.

kuwa na huruma kwao

"kuwa na huruma kwao"

Psalms 106:47

Taarifa ya Jumla

Hapa 106.48 ni zaidi ya mwisho wa zaburi. NI kauli ya kufunga kwa kitabu chote cha 4 cha Zaburi, ambacho kinaanaza katika Zaburi 90 na kukamilika na Zaburi 106.

Na Yahwe Mungu wa Israeli asifiwe

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Na watu wamsifu Yahwe Mungu wa Israeli"

kwa jina lako takatifu

Hapa Yahwe ina maana ya "jina lake takatifu". "kwako"

kutoka milele mpaka milele

Hii ina maana ya tofauti kubwa na ina maana ya muda wote. "kwa milele yote"

Psalms 107

Psalms 107:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

uaminifu wa agano lako huduma milele

"upendo wake wa uaminifu kwangu hautaisha"

waliokombolewa na Yahwe

"Waliokombolewa" inamaanisha watu ambao Yahwe amewaokoa. "wale ambao Yahwe amewaokoa"

waongee

Hii inamaanisha kuwaambia wengine kuhusu kitu. "waambie yale Yahwe aliyofanya"

kutoka mkono wa adui

Hapa "mkono" unamaanisha nguvu. "kutoka kwenye nguvu ya adui"

kutoka mashariki ... na kutoka kusini

Hapa pande nne zinatolewa kusisitiza kwamba atawakusanya kutoka kila sehemu. "kutoka kila upande" au "kutoka kila sehemu ya dunia"

kutoka mashariki na kutoka magharibi, kutoka kaskazini na kutoka kusini

Hii inafafanua sehemu ambapo Yahwe anawakusanyia watu wake. "amewakusanya kutoka mashariki na kutoka magharibi, kutoka kaskazini na kutoka kusini"

Psalms 107:4

walizurura

"Baadhi ya watu walizurura"

katika njia ya jangwani

"kwenye barabara lililokuwa jangwani"

wakuishi

"Ambayo wanliweza kuishimo"

Kisha wakamuita Yahwe katika shida yao

Inaashiriwa kuwa wanaomba kwa Yahwe ili awasaidie. "Kisha wakaomba kwa Yahwe kuwasaidia katika shida yao"

dhiki

"tabu" au "mateso"

Psalms 107:8

O watu wamsifu Yahwe kwa uaminifu wake wa agano

"Acha watu wamsifu Yahwe kwa sababu anawapenda kwa uaminifu" au "Watu wanapaswa kumsifu Mungu kwa sababu ya upendo wake wa uaminifu." Hapa neno "O" linatumika kuonesha hamu kubwa ya watu kumsifu.

wanadamu

"watu"

Kwa kuwa anaridhisha hamu za wale walio na kiu

"Kwa kuwa anawapa maji wanaotamani - kwa wale walio na kiu"

na hamu za wale walio na njaa anawajaza na vitu vizuri

"na kwa wale walio na njaa sana na hamu ya chakula, anawapa vitu vizuri vya kula"

kwa wanadamu

"kwa watu wote"

Baadhi waliketi

Inadokezwa kwamba hawa ni watu ambao Yahwe aliwaokoa. "Yahwe pia aliwaokoa watu walioketi"

gizani na kwenye utusitusi

"Gizani" na "utusitusi" zina maana sawa na zinatumika kusisitiza jinsi gereza lilivyokuwa giza. "katika giza kabisa"

Psalms 107:11

waliasi dhidi ya neno la Mungu ... kukataa maagazi ya Aliye juu.

Misemo hii ina maana sawa na inasisitiza jinsi walivyomuasi Mungu, ambayo ndio sababu ya kufungwa.

Alinyenyekesha mioyo yao kupitia ugumu

Hapa moyo unamaanisha mtu, lakini mahususi mapenzi yake. "Aliwanyenyekesha kwa kuwaruhusu wapitie magumu"

ugumu

Maana zinazowezekana ni 1) "tabu" au 2) "kazi ngumu"

walijikwaa na hakuwepo mtu kuwasaidia kuinuka

Neno "kujikwaa" linamaanisha wakati watu hawa walijikuta kwenye nyakati ngumu sana. "waliingia taabuni na hakuwepo mtu wakuwakomboa"

Kisha wakamuita Yahwe katika tabu yao

Inaashiriwa kuwa wanaomba kwa Yahwe ili awasaidie. "Kisha wakaomba kwa Yahwe kuwasaidia katika shida yao"

dhiki yao

"taabu" au "mateso"

akawatoa

Hapa Daudi anaelezea Yahwe kuwaokoa kutoka dhiki yao kana kwamba dhiki ilikuwa sehemu ya kimwili ambayo alikuwa akiwatoa.

Psalms 107:14

Akawatoa

"Yahwe akawaleta wale walikuwa gerezani"

gizani na kwenye utusitusi

"Gizani" na "utusitusi" zina maana sawa na zinatumika kusisitiza jinsi gereza lilivyokuwa giza. "katika giza kabisa"

O watu wamsifu Yahwe kwa uaminifu wake wa agano

"Acha watu wamsifu Yahwe kwa sababu anawapenda kwa uaminifu" au "Watu wanapaswa kumsifu Mungu kwa sababu ya upendo wake wa uaminifu." Hapa neno "O" linatumika kuonesha hamu kubwa ya watu kumsifu.

Kwa kuwa

"Kwa sababu"

Kwa kuwa amevunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma

Misemo hii miwili inaelezea Yahwe anavyowafungua watu kutoka gerezani na inatumika kusisitiza kwamba Yahwe kweli aliwaweka huru. "Aliwaweka huru watu wake kutoka gerezani"

Psalms 107:17

Walikuwa wapumbavu katika njia zao za uasi

"Walikuwa wapumbavu jinsi walivyoasi dhidi ya Yahwe"

na kuteswa

"na waliteseka." Kwa bayaba waliteseka kwa kuugua. "na wakawa wagonjwa"

wakaja karibu na malango ya kifo

Hapa tendo la "kufa" linaelezwa kama sehemu, "malango ya kifo" "kidogo wafe"

Kisha wakamuita Yahwe katika tabu yao

Inaashiriwa kuwa wanaomba kwa Yahwe ili awasaidie. "Kisha wakaomba kwa Yahwe kuwasaidia katika shida yao"

Psalms 107:20

Alituma neno lake na kuwaponya

Hapa Daudi anaeleza Yahwe kuzungumza kama kutuma maneno yake kana kwamba yalikuwa mjumbe. Maana zinazowezekana ni 1) "Aliamuru waponywe na wakaponywa" au 2) "Aliwatia moyo na kuwaponya"

O watu wamsifu Yahwe kwa uaminifu wake wa agano

"Acha watu wamsifu Yahwe kwa sababu anawapenda kwa uaminifu" au "Watu wanapaswa kumsifu Mungu kwa sababu ya upendo wake wa uaminifu." Hapa neno "O" linatumika kuonesha hamu kubwa ya watu kumsifu.

ya shukrani

"zinazoonesha kuwa wanashukuru"

kwa kuimba

"kwa kuimba kuyahusu"

Psalms 107:23

na kufanya biashara ng'ambo

Walikuwa wakisafari sehemu za ng'ambo na kununua na kuuza vitu na watu huko. "kuuza vitu kwenye miji ya mbali"

Psalms 107:25

aliamuru na kuamsha dhoruba unaotikisa bahari

"aliamuru upepo na kuusababisha kuwa dhoruba kubwa iliyolitikisa bahari"

dhoruba

upepo wenye nguvu nyingi sana ambao mara nyingi unaambatana na mvua kali

unaotikisa bahari

Hapa Daudi anaelezea upepo unaosababisha mawimbi kuwa juu kana kwamba mawimbi ni kitu kinachokoroga kitu kwa nguvu. ""uliosababisha mawimbi ya baharini kuwa juu sana"

Wakafika juu mbinguni; wakashuka chini vilindini

Hii inaelezea kuinuka na kushuka kwa meli na mawimbi. Kupanda juu kabisa hadi mawinguni na kushuka chini kwenye vilindi ni kukuza maneno ili kuonesha jinsi dhoruba ilivyokuwa mbaya. "meli zao ziliinuka juu sana kwenye mawimbi na kisha kudondoka chini sana katikati ya mawimbi"

Maisha yao yaliyeyuka kwa dhiki

Lugha hii inaelezea uoga wa mabaharia. "Wanaume waliogopa sana na kuwa na dhiki sana"

walikuwa wamechanganyikiwa

Msemo "kuchanganyikiwa" unamaanisha hawakujua nini cha kufanya. "na hawakujua chakufanya." au "hawakuwa na wazo la nini cha kufanya"

Psalms 107:28

Kisha wakamuita Yahwe katika tabu yao

Inaashiriwa kuwa wanaomba kwa Yahwe ili awasaidie. "Kisha wakaomba kwa Yahwe kuwasaidia katika shida yao"

Kisha waka...

Wanaozungumziwa hapa ni mabaharia.

Akatuliza dhoruba

"Akafanya upepo ukome"

mawimbi yakatulia

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "akafanya mawimbi yatulie"

akawaleta

"akawaongoza"

bandari waliyotaka

"kwenye bandari waliotaka kwenda"

Psalms 107:31

O watu wamsifu Yahwe kwa uaminifu wake wa agano

"Acha watu wamsifu Yahwe kwa sababu anawapenda kwa uaminifu" au "Watu wanapaswa kumsifu Mungu kwa sababu ya upendo wake wa uaminifu." Hapa neno "O" linatumika kuonesha hamu kubwa ya watu kumsifu.

wamsifu katika baraza la wazee

"wazee wanapokaa pamoja." Wazee waliketi pamoja kuzungumzia maswala ya jamii na kufanya maamuzi kwa ajili ya jamii.

Psalms 107:33

Anageuza

"Yahwe anafanya"

kwa sababu ya uovu wa watu wake

"kwa sababu watu wanaoishi hapo ni waovu"

Anageuza jangwa kuwa bwawa la maji na nchi kavu kuwa chechemi za maji

Misemo hii yote miwili ina maana ya kufanana na inasisitiza jinsi Yahwe anavyofanya maji yatokee jangwani. "Hufanya chemchemi na maziwa katika ardhi iliyokuwa jangwa"

Psalms 107:36

Anawatuliza walio na njaa huko

Hapa neno "huko" linamaanisha sehemu ambazo Yahwe alifanya chechemi na maziwa kutokea. Pia msemo "walio na njaa" inamaanisha watu walio na njaa. "Yahwe anafanya watu walio na njaa kuishi huko"

kupanda mashamba ya mizabibu

"ya kupandia mizabibu"

na kuleta mavuno tele

"ili walete mavuno tele"

kwa hiyo wanakuwa wengi sana

"ili watu wao wawe wengi sana"

Haachi ng'ombe wake wapungue idadi

Hii inaweza kuelezwa katika hali chanya. "Huweka ng'ombe wao kuwa wengi sana"

Psalms 107:39

Walipunguzwa

Wanaozungumziwa hapa ni watu waliokuwa na njaa na Yahwe kuwatuliza katika nchi. Sentensi hii inaeleza jinsi walivyokuwa kabla ya Yahwe kuwatuliza katika nchi.

Walipunguzwa na kuletwa chini

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. Viongozi wao walipunguza idada yao na kuwaleta chini"

Walipunguzwa

"wakawa wachache kwa idadi"

kuletwa chini

Hiiinamaanisha kuaibishwa. "kuaibishwa"

Humwaga dharau

Hapa Daudi anazungumzia Yahwe kuwaonesha dharau viongozi kana kwamba dharau ni kuletwa chini alichowamwagia. "kuwaonesha dharau"

kwa viongozi

"wakubwa." Hii namaanisha viongozi waliowakandamiza watu. "viongozi waliowakandamiza"

ambapo hakuna mabarabara

"ambapo watu hawaendi"

Psalms 107:41

Lakina ana...

"Lakini Yahwe"

wahitaji

Hii inamaanisha watu wahitaji. "watu wahitaji" au "watu maskini"

hujali familia zake kama kundi

Hapa Daudi analinganisha jinsi Yahwe anavyowajali watu wake na jinsi mchungaji anavyojali kondoo wake. Maana zinazowezekana ni 1) "hufanya idadi ya watu kwatika famila zao kuongezeka kama kundi" au 2) "huwajali kama mchungaji anavyojali kondoo wake"

Wanyofu

Hii inamaanisha watu wanaoishi maisha ya unyofu. "Watu wanyofu" au "Watu wanaofanya kilicho sawa"

uovu wote

Hapa watu waovu wanazungumziwa kama "uovu." "watu wote waovu"

huziba mdomo

hii inamaanisha kutokujibu kitu. "hana kitu cha kumjibu Yahwe"

ayaangalie mambo haya yote

Hii namaanisha kuwaza vitu hivi. "kuwaza kuhusu hivi vitu" au "kukumbuka hivi vitu"

Psalms 108

Psalms 108:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Moyo wangu uko thabiti, Mungu

Hapa Daudi anajitambulisha kwa moyo wake. Pia, neno "thabiti" inamaanisha kuamini kabisa. "Moyo wangu uko thabiti kwako, Mungu" au "Nakuamini wewe kabisa, Mungu"

Nitaimba sifa pia na moyo wangu uliotukuzwa

Hapa Daudi anajitambulisha kama kuwa na heshima ya kumsifu Mungu. "Unaniheshimu kwa kuniruhusu kukuimbia sifa"

Amka, kinanda na kinubi

Hapa Daudi anaeleza kucheza vyombo kama kutembea kutoka usingizini. "Nitakusifu kwa kucheza kinanda na kinubi"

Nitaamsha alfajiri

Hapa Daudi anaeleza alfajiri kuamka kama mtu kuamka asubuhi. "Nitakuwa nikikusifu alfajiri ifikapo"

alfajiri

jua linapochomoza.

Psalms 108:3

Kwa kuwa uaminifu wako wa agano ni mkuu ... uaminifu wako unafika mawinguni

Misemo hii miwli ina maana ya kufanana. Inalinganisha ukuu wa uaminifu wa agano wa Yahwe na uaminifu wake kwa ukuu wa jinsi mbingu zilivyo juu ya nchi. "uaminifu wako wa agano na uaminifu wako ni zaidi ya umbali kati ya mbingu na nchi"

Psalms 108:5

Utukuzwe Mungu, juu ya mbingu

Mwandishi wa zaburi anamuomba Mungu kuonesha kuwa ametukuzwa. Kutukuzwa juu ya mbingu inaonesha kuwa mkuu. "Mungu, onesha kuwa umetukuzwa juu ya mbingu" au "Mungu, onesha kuwa umetukuzwa juu ya mbingu" au "Mungu, onesha kuwa wewe ni mkuu mbinguni"

utukufu wako uinuliwe

Hapa Yahwe anaoneshwa kwa "utukufu" wake. "utukuzwe"

Ili wale uwapendao waokolewe

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Kwa sababu wale uwapendao wanahitaji kuokolewa" au "Okoa wale unaowapenda"

kwa mkono wako wa kuume

Hapa "mkono wa kuume" wa Yahwe unamaanisha nguvu yake. "kwa nguvu yako"

nijibu

Kumjibu hapa inamaanisha kujibu ombi lake. "jibu ombi langu"

Psalms 108:7

Mungu amezungumza katika utakatifu wake

Hapa Daudi anaeleza Mungu kusema kitu kwa sababu ni mtakatifu kama kuzungumza "katika utakatifu wake," kana kwamba utakatifu wake ni kitu ambacho yuko ndani yake. "Mungu, kwa sababu ni mtakatifu, amesema"

Nitaigawa Shekemu na kuligawa bonde la Sukothi

Hapa Mungu anazungumza kuhusu kuigawa nchi ya Shekemu na bonde la Sukothi.

kugawa

kugawa katika vipande

Efraimu ni kofia yangu pia

Mungu analizungumzia kabila la Efraimu kana kwamba lilikuwa jeshi lake. Kofia ya chuma inaashiria kifaa cha vita. "Efraimu ni kama kofia ya chuma niliochagua kwa ajili ya vita" au "Kabila la Efraimu ni jeshi langu"

kofia ya chuma

Kofia ngumu ambayo askari huvaa kulinda vichwa vyao dhidi ya majeraha.

Yuda ni fimbo yangu

Mungu alichagua watu kutoka kabila la Yuda kuwa wafalme wa watu wake, na analizungumzia hilo kabila kama vile ni fimbo yake. "Kabila la Yuda ni kama fimbo yangu" au "Yuda ni kabila ambayo natawalia watu wangu"

Psalms 108:9

Moabu ni bakuli langu la kunawia

Mungu anaizungumzia Moabu kutokuwa muhimu kana kwamba Moabu ilikuwa bakuli la kunawia au mtumishi wa chini sana. "Moabu ni kama bakuli ninalotumia kunawa"

juu ya Edomu niturusha kiatu changu

Inawezekana kwamba Mungu alikuwa akizungumzia kuimiliki Edomu kana kwamba alikuwa akitupa kiatu chake kama ishara ya kuonesha kuwa anapamiliki. Lakini matoleo mengine yana tafsiri tofauti. "Ninaimiliki nchi ya Edomu" au "Ninarusha kiatu changu katika nchi ya Edomu kuonesha kuwa ni yangu"

Psalms 108:11

Taarifa ya Jumla:

lakina angalia kuwa 108:11 haina maneno "Lakini wewe," kama mwanzo wa 60:10.

Mungu, je haujatukataa?

Mwandishi wa zaburi anatumia swali hili kuonesha huzuni yake kwamba inaonekana Mungu amewakataa. "Inaonekana kama umetukataa" au "Mungu, unaonekana kututelekeza"

Hauendi vitani na jeshi letu

Mwandishi wa zaburi anazungumzia Mungu kulisaidia jeshi lao kana kwamba Mungu alikuwa akienda kupiga pamoja nao. "haulisaidii jeshi letu tunapoenda kupambana"

hauna maana

"batili"

tutashinda

kuwa na ushindi

atawakanyaga chini adui zetu

Mwandishi wa zaburi anamzungumzia Mungu kusaidia jeshi lao kuwashinda maadui kana kwamba Mungu alikuwa wa kuwaganyaga chini maadui." "atatuwezesha kuwakanyaga chin maadui" au "atatufanya tuweze kuwashinda maadui wetu"

Psalms 109

Psalms 109:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Kwa waovu na waongo

Maneno "uovu" na "uongo" inamaanisha watu. Zina maana yakufanana na inasisitiza jinsi watu hawa walivyo waovu. "Kwa wanaume waovu na waongo"

Psalms 109:4

Baada ya upendo wangu wananikashifu

"Ingawa niliwapenda, wananishtaki"

upendo wangu

"upendo wangu kwao"

wananikashifu

Wanaomkashifu ni wale watu waovu na waongo.

Psalms 109:6

Weka mtu mwovu ... weka mshitaki

Misemo hii miwili iko sambamba na misemo "mtu mwovu" na "mshitaki" inamaanisha mtu yule yule.

kwenye mkono wake wa kuume

"kwenye mkono wake wa kuume wa adui yangu"

Akihukumiwa, akutwe na hatia

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Anapokuwa anashtakiwa, hakimu ampate na hatia"

maombi yake yafikiriwa kuwa ya dhambi

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "fikiria maombi yake kama dhambi"

Psalms 109:8

Siku zake ziwe chache

Usemi huu "Siku zake" unamaanisha urefu wa maisha yake. "Asiishi maisha marefu"

ofisi yake

"nafasi yake ya mamlaka"

misaada

chakula au fedha inayopewa kwa ombaomba

nyumba zao zilizoharibika

"waliangamiza nyumba"

Psalms 109:11

Mdai

mtu anayeazimisha fedha kwa mtu mwingine lakini anategemea huyo mtu alimpe.

wapore

"waibe"

Watoto wake wakatwe; jina lao lifutwe

Misemo hii miwili inamaana ya kufanana na inasisitiza watoto wake kuangamizwa.

Watoto wake wakatwe

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Kusababisha watoto wake kukatwa" au "Kusababisha watoto wake kufa"

jina lao lifutwe katika kizazi kijacho

Hapa wazo la kutokuwepo na mtu kuendeleza jina la familia inazungumziwa kama "jina lao kufutwa." "asiwepo mtu kuendeleza jina lake"

Psalms 109:14

Dhambi za mababu yake zitajwe kwa Yahwe

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Na ukumbuke dhambi za mababu zake, Yahwe"

na dhambi ya mama yake isisahaulike

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Na usisahau dhambi ambazo mama yake alitenda"

Na hatia yao daima iwe mbele ya Yahwe

Hapa Daudi anazungumzia Yahwe kuwaza kuhusu hatia yao kana kwamba hatia yao ni kitu cha kimwili kilicho mbele yao. "Na Yahwe aendelee kufikiria kuhusu dhambi zao"

Yahwe akate kumbukumbu yao kutoka duniani

Daudi anatumia neno "dunia" kumaanisha watu wote wanaoishi duniani. Pia, msemo "kumbukumbu yao" inamaanisha watu kuwakumbuka baada ya kufa. "na Yahwe afanye kwamba watu duniani wasiwakumbuke"

mtu huyu hajawahi kuhangaika kuonesha uaminifu wowote wa agano

Hii inamaanisha yeye kuonesha uaminifu wa agano kwa watu. "mtu hakuhangaika kuonesha uaminifu wa agano kwa watu"

waliokandamizwa, wahitaji

Hii inamaanisha watu waliokandamizwa na wahitaji. "watu waliokandamizwa, watu wahitaji"

waliovunjika moyo

Hii inamaanisha watu waliovunjika moyo. "watu waliovunjika moyo" au "watu waliokata tamaa"

hadi kifo

"hadi wafe." Hii inamaanisha kuwa aliwatesa hadi walipokufa.

Psalms 109:17

na imrudie juu yake

"laana zake zije juu yake"

Alijivika kwa kulaani kama vazi lake

Daudi anazungumzia tabia ya mtu mwovu kana kwamba ni vazi lake. "Aliwalaani watu wengine mara nyingi kama avaavyo nguo. au "Aliwalaani watu muda wote"

kama vazi lake

"kana kwamba yalikuwa mavazi yake"

laana ikaja kwake kama maji, kama mafuta kwenye mifupa yake

Maana zinazowezekana ni: 1) Alizungumza laana sana hadi zikawa sehmu ya utambulisho wake. "laana anazozungumza ni sehemu yake alivyo" au 2) laana alizozizungumza zilimtokea yeye. "yeye mzima alilaaniwa kwa laana aliyozungumza"

kama maji

Hii inamaanisha jinsi mtu alivyokunywa maji. "kama maji ambayo mtu hunywa"

kama mafuta kwenye mifupa yake

Hii inamaanisha jinsi mafuta yanavozama kwenye mifupa yanapopakwa kwenye ngozi. "kama mafuta ya mzeituni yanavyozama kwenye mifupa ya mtu yanapopakwa kwenye ngozi yake"

Psalms 109:19

Laana zake ziwe kwake kama nguo avaazo kujifunika

Watu walivaa nguo zao kila siku. Daudi anamzungumzia yeye kufunikwa na laana kama kufunikwa na nguo. "Acha laana zake ziwe juu yake kila siku kama nguo avaazo"

kama mshipi ambao hua huvaa

Maneno haya yanaweza kuongezwa. "na acha laana zake daima ziwe juu yake kama mshipi auvaao"

Na hii iwe dhawabu yake

"Na laana hizi ziwe dhawabu yake"

Psalms 109:21

unitendee kwa fadhila

Hili ni ombi kwa Yahwe kumtendea kwa fadhila. "nitendee kwa fadhili"

kwa ajili ya jina lako

"kwa ajili ya sifa yako"

nimekandamizwa na muhitaji

Maneno haya mawili yana maana ya kufanana na yanasisitiza kuwa hawezi kujisaidia.

moyo wangu umeumia ndani yangu

Hapa daudi anazungumzia kukata tamaa kama moyo wake kuumia. "nimejaa majonzi na kukata tamaa"

Ninafifia kama kivuli ... kama nzige

Daudi anahisi kama anataka kufa na anaeleza hisia hii kwa kujifananisha na kivuli kinachofifia na jinsi upepo unavyopuliza nzige. "Nahisi kama nataka kufa, kama kivuli cha jioni kitakacho potea punde, kama nzige anavyopulizwa kirahisi na upepo"

Psalms 109:24

Magoti yangu yamechoka

Hii inamaanisha kuwa ameishiwa nguvu na vigumu kwake kusima. "Nina wakati mgumu kusima" au "Mwili wangu umechoka"

kutokana na kufunga

"kwa sababu sili chakula chochote"

Ninageuka kuwa ngozi na mifupa

Hii inamaanisha amepoteza uzito mwingi. "mwili wangu umekonda sana"

Ninadharauriwa na washtaki wangu

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "washtaki wangu wananidhihaki"

wanatikisa vichwa vyao

Hili ni tendo la kutokukubali.

Psalms 109:26

Na wajue

Wanaozungumziwa ni washtaki wa Daudi na watu wanaosema vitu vibaya kumhusu.

umefanya hili

"umeniokoa"

Psalms 109:28

Ingawa wananilaani

Wanaozungumziwa ni watu wanaomshtaki Daudi na kusema vitu vibaya kumhusu.

na waaibishwe

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "na waaibike" au "acha waaibike"

lakini watumishi wako wafurahi

"lakini mimi, mtumishi wako, nifurahi" au "mimi ni mtumishi wako, acha nifurahi." Daudi anatumia msemo "mtumishi wako" kumaanisha ni yeye.

Na washindani wangu wavikwe ... na wavae

Misemo hii miwili ina maana ya kufanana na inatumika kusisitiza jinsi anavyotamani sana waaibishwe.

wavikwe aibu

Hapa Daudi anawazungumzia kuaibika kana kwamba ilikuwa vazi walilovaa. "waaibike sana"

na wavae aibu yao kama joho

Daudi anawazungumzia kuaibika kana kwamba ilikuwa joho walilovaa. "na aibu yao iwafunike kama joho walilojifunika"

Psalms 109:30

Kwa mdomo wangu natoa

Hii inamaanisha kuwa atazungumza. "Nitazungumza na kutoa"

atasimama mkono wa kuume wa yule aliye mhitaji

Hii inamaanisha atamsaidia na kumtetea mtu maskini. "atamtetea mtu aliye mhitaji"

Psalms 110

Psalms 110:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Keti mkono wangu wa kuume

Msemo "mkono wangu wa kuume" unamaanisha sehemu ya heshima. "Keti sehemu ya heshima niliyokuandalia"

niwaweke adui zako chini ya miguu yako

Hapa Dauddi anamuelezea Yahwe kuwaweka adui wa bwana wake chini ya uwezo na mamlaka yake kama kuwaweka chini ya miguu yake. "umewaweka adui zako chini ya uwezo wako"

Psalms 110:2

Taarifa ya jumla:

Daudi anaendelea kuzungumza na mfalme

Yahwe ataishikilia fimbo ya nguvu yako

Hapa Daudi anamzungumzia Yahwe kupanua eneo analotawala mfalme kama kushikilia fimbo yake. "Yahwe atapanua eneo ambalo unatawala kwa uwezo"

tawala juu ya adui zako

"Mfalme, tawala kati ya adui zako." Hii inasemwa kwa mfalme kama amri.

kwa hiari yao wanyewe

"kwa uamuzi wao." Hii inamaanisha watachagua kumfuata mfalme.

katika siku ya uwezo wako

Hii inamaanisha siku ambayo mfalme atawaongoza watu wake vitani. Hii inaweza kuelezwa wazi. "katika siku utakapoliongoza jeshi lako vitani"

kutoka tumbo la alfajiri ... kama umande

Daudi anaelezea umande kama mtoto ambaye anazaliwa na umande. "asubuhi ... kama umande"

kutoka tumbo la alfajiri ujana wako utakuwa kwako kama umande

Daudi anamwambia mfalme kuwa atakuwa na nguvu za ujana kila asubuhi kwa kumfananisha na jinsi umande unavyotokeza mapema kila asubuhi. "kila asubuhi utajazwa na nguvu za ujana kukuhimili kama kila asubuhi umande unavyotokea kumwagilia na kuhimili ardhi"

Psalms 110:4

Wewe ni

Yahwe anazungumza na bwana.

hautabadilika

Hii inamaanisha kwamba hatabadili alichosema. "hatabadili mawazo yake" au "hatabadili alichosema"

baada ya mfano wa Melkizedeki

Maneno yasiyokowepo yanaweza kuongezwa. "baada ya mfano alivyokuwa kuhani Melkizedeki" au "katika njia ile ile alivyokuwa kuhani Melkizedeki"

Psalms 110:5

Bwana yu mkono wako wa kuume

Bwana anapokwenda vitani, Yahwe husimama mkono wake wa kuume ili kumsaidia. "Bwana anakusaidia vitani"

Bwana

Neno "Bwana" linamaanisha Yahwe.

Atawaua

Atakaye waua ni Yahwe. Atasababisha wafalme washindwe na kufa, lakini ataruhusu majeshi ya mfalme kuwaua waflame maadui. "Atasababisha wafalme wafe" au "Ataruhusu jeshi lako liwaue wafalme wote"

wafalme

Hii inamaanisha adui zake. "wafalme adui"

katika siku ya hasira yake

Hapa Daudi anazungumzia siku ambayo Yahwe atakasirika na kuwaangamiza wafalme kama "siku ya hasira yake." "katika siku ya hukumu ambapo uvumilivu wake utageuka kuwa hasira"

atajaza viwanja vya mapambano na miili iliyokufa

Hii inamaanisha kuwa Yahwe atasababisha hiki kitokee, sio kwamba atawaua watu wote mwenyewe watakaokufa vitani. "atasababisha viwanja vya mapambano kujazwa na miili iliyokufa"

atawaua viongozi katika nchi nyingi

Hii inamaanisha kuwa Yahwe atasababisha hiki kitokee, sio kwamba atawaua viongozi wenyewe. "atasababisha viongozi katika nchi nyingi kuuawa" au "ataruhusu viongozi katika nchi nyingi kufa"

Psalms 110:7

Atakunywa kwenye kijito njiani

Mfalme anasimama kidogo tu kwa ajili ya kinywaji na kisha anaendelea kuwafuatilia adui zake. "Akiwa anawafuatilia adui zake, atasimama tu kunywa kwenye kijito"

kwenye kijito

Hii inamaanisha kuwa atakunywa maji kutoka kwenye kijito. Kijito ni mto mdogo. "atakunywa maji kutoka kwenye kijito"

na kisha

"kwa hiyo"

atainua kichwa chake

Maana zinazowezekana ni 1) mfalme anainua kichwa chake mwenyewe au 2) Yahwe anainua kichwa cha mfalme.

atainua kichwa chake juu baada ya ushindi

Watu waliinua vichwa vyao walipokuwa washindi, walipojiamini na walipokuwa wenye furaha. "atainua kichwa chake kwa kujiamini baada ya ushindi" au "atakuwa mshindi"

Psalms 111

Psalms 111:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kihebrania.

kwa moyo wangu wote

Hapa neno "moyo" inawakilisha mtu kamili na hisia. "kwa kila kitu nilivyo"

katika kusanyiko la wanyofu, katikati yao

Misemo hii miwili inamaanisha kitu kimoja na inaweza kuunganishwa kama ikihitajika. "katika mkusanyiko wa watu wanyofu"

yanasubiriwa kwa hamu na wale wote wanaoyatamani

Yanaosubiriwa ni "matendo ya Yahwe." HIi inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "wale wote wanaotamani kazi za Yahwe wanasubiri kwa hamu"

yanasubiriwa kwa hamu

Maana zinazowezekana ni 1) "kutafuta" au 2) "kusoma"

Psalms 111:4

ambayo yatakumbukwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "ambayo watu watakumbuka daima"

atakumbuka

"ataitisha akilini"

matendo yake makuu

"matendo yake yaliyoonesha nguvu yake"

urithi wa mataifa

Mwandishi anazungumzia nchi iliyokuwa ya mataifa ya Kanaani kana kwamba ilikuwa urithi wao. "nchi iliyokuwa ya mataifa mengine"

Psalms 111:7

Kazi za mikono yake

Hapa neno "mikono" inamaanisha Yahwe, mwenyewe. "Kazi anazofanya"

Imethibitika milele

Hii inamaanisha kuwa maelezo ya Yahwe hayabadiliki na yanadumu milele. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Amezithibitisha milele" au "Zitadumu milele"

kuangaliwa kwa uaminifu na vizuri

Maana zinazowezekana ni 1) Yahwe ametoa maelezo yake katika namna ya uaminifu na iliyo sawa au 2) watu wake wanapaswa kuangalia maelezo ya Yahwe kwa namana ya uaminifu na iliyo sawa. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "kwa watu wake kuziangalia kwa uaminifu na vizuri"

mtakatifu na la ajabu ni jina lake

Hapa neno "jina" linamaanisha Yahwe mwenyewe. "Yahwe ni mtakatifu na waajabu"

Psalms 111:10

mwanzo wa hekima

Neno "hekima" inaweza kutafsiriwa kama kitenzi. "hatua ya kwanza ya kuwa na hekima" au "kitu muhimu zaidi kuwa na hekima"

wale wanaobeba maelekezo yake

"wale wanaotii maelezo yake"

Sifa yake huduma milele

Neno "sifa" inaweza kutafsiriwa kama kitenzi. "Watu watamsifu milele"

Psalms 112

Psalms 112:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

anayefurahi sana

"unafurahia sana"

uzao wa mnyofu utabarikiwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe ataubariki uzao wa mtu mnyofu"

Psalms 112:3

Taarifa ya Jumla:

Mtu anayeimba wimbo huu anaendelea kumwelezea mtu anaye mheshimu sana Yahwe.

Mali na utajiri uko nyumbani mwake

Hapa neno "nyumba" inamaanisha familia. Maneno "Mali" na "utajiri" yanamaanisha kitu kimoja na yanaashiria utajiri mkubwa. "Familia yake ilikuwa tajiri sana"

Nuru hung'aa gizani kwa ajili ya mtu mnyofu

Mwandishi anamzungumzia Mungu kumbariki mtu mnyofu katika nyakati ngumu kana kwamba ilikuwa ni nuru inang'aa gizani. "Baraka ambayo mtu mnyofu anapokea kutoka kwa Mungu ni kama nuru inayong'aa gizani"

hukopesha fedha

Taarifa inaweza kuwekwa wazi. "anakopesha fedha zake kwa watu wengine."

Psalms 112:6

Taarifa ya Jumla:

Mtu anayeimba wimbo huu anaendelea kumwelezea mtu anaye mheshimu sana Yahwe.

Kwa kuwa hatasogezwa

hatasumbuliwa au kuzidiwa kwa hali yoyote kwa kuwa imani yake iko katika Yahwe. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "kwa kuwa hakuna kitu kitakachomsogeza"

kwa kuwa mtu mwenye haki atakumbukwa milele

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "watu watamkumbuka mtu mwenye haki milele"

Psalms 112:8

Taarifa ya Jumla:

Mtu anayeimba wimbo huu anaendelea kumwelezea mtu anaye mheshimu sana Yahwe.

Moyo wake ni tulivu

"Moyo wake umethibitika." Hapo neno "moyo" inaashiria mtu. Maana zinazowezekana ni 1) "yuko na amani" au 2) "Anajiamini"

haki yake hudumu milele

"matendo yake yatadumu milele."

atatukuzwa na heshima

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe atamtukuza kwa kumpa heshima"

Psalms 112:10

ataona hili

"ataona kuwa vitu vinaenda vizuri kwa mtu mnyofu." Neno "hili" linamaanisha kila kitu kizuri ambacho mwandishi alieleza katika mstari ulipoita kuhusu mtu mnyofu.

atasaga meno

Kusaga meno ilikuwa ni ishara ya daharu.

kuyeyuka

Mwandishi anamzungumzia hatima ya kifo cha mtu mwovu kana kwamba huyo mtu ni kitu, kama barafu inayoweza kuyeyuka. "hatimaye atakufa"

hamu ya watu waovu itaangamia

Maana zinazowezekana za "hamu" ni 1) hamu ya kihisia waliyo nayo watu waovu. "vitu ambavyo watu waovu wanataka kufanya havitawahi kutokea" au 2) ni njia nyingine yakusema vitu ambavyo watu waovu wanatamani. "watu waovu watapoteza vitu wanavyotamani"

Psalms 113

Psalms 113:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

jina la Yahwe

Hapa neno "jina" linamaanisha Yahwe mwenyewe. "Yahwe"

Psalms 113:3

Kutoka maawio ya jua hadi kuzama kwake

Hii inamaanisha upande wa mashariki ambapo jua linachomoka, na magharibi, ambapo jua linazama. Mwandishi anatumia tofauti hizi kuashiria kila sehemu duniani. "Kila sehemu duniani"

Jina la Yahwe linapaswa kusifiwa

Hapa neno "jina" linamaanisha Yahwe mwenyewe. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "watu wanapaswa kumsifu Yahwe"

utukufu wake unafika juu ya mbingu

Utukufu wa Mungu unazungumziwa kana kwamba ulikuwa juu sana. "utukufu wake uko juu zaidi ya mbingu" au "utukufu wake ni mkuu sana"

Psalms 113:5

Ni nani kama Yahwe Mungu wetu ... duniani?

Mwandishi anauliza swali kusisitiza kuwa hakuna mtu kama Yahwe. Hili swali la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Hakuna kama Yahwe Mungu wetu ... duniani."

aliye na kiti chake juu

"aliyesimikwa juu" au "anayetawala katika nafasi ya juu zaidi"

Psalms 113:7

Anawainua maskini ... kutoka kwenye lundo la

Misemo hii miwili ina usambamba. Mwandishi anamzungumzia Yahwe kuwasaidia na kuwatukuza watu walio maskini kana kwamba Yahwe aliwasababisha kusimama kutoka kuketi kwenye vumbi na majivu.

kutoka mavumbini ...kutoka kwenye lundo la majivu

Kukaa kwenye mavumbi au majivu kunaashiria kati ya umaskini au kukata tamaa.

ili aketi na wakuu , na wakuu wa watu wake

Hapa msemo wa pili unaewka wazi kuwa msemo wa kwanza unamaanisha wakuu wa watu wa Yahwe. Misemo hii miwili inaweza kuunganishwa. "ili Yahwe amkalishe pamoja na wakuu wa watu wake"

Psalms 113:9

Anampa nyumba mwanamke aliyetasa

Hapa "nyumba" inamaanisha watoto wanaoishi nyumbani. "Anampa watoto mwanamke ambaye hakuwanao"

Psalms 114

Psalms 114:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Israeli iliondoka Misri, nyumba ya Yakobo kutoka kwa wageni

Mistari hii miwili ina usambamba, "Israeli" na "nyumba ya Yakobo" inamaanisha kitu kimoja na "Misri" na "watu wageni" inamaanisha watu wale wale.

nyumba ya Yakobo kutoka kwa wageni

Neno "nyumba" hapa linamaansiha familia au uzao. Kitenzi kinaweza kuwekwa kwa ajili ya huu msemo. "uzao wa Yakobo ukaondoka kutoka kwa watu wageni"

Yuda pakawa mahali pake patakatifu, Israeli ufalme wake

Maana zinazowezekana kwa ajili ya "Yuda" na "Israeli" ni 1) zinamaanisha nchi. "Nchi ya Yuda ikawa sehemu takatifu ya Yahwe, nchi ya Israeli ikawa ufalme wake" au 2) ni njia nyingine ya kusema watu wa Yuda na Israeli. "Watu wa Yuda wakawa miongoni mwa wale ambapo Yahwe aliishi, watu wa Israeli wakawa wale ambao aliwatala"

Psalms 114:3

Bahari lilitazama na kutoroka

Mwandishi anazungumzia bahari la Matete kana kwamba lilikuwa ni mtu aliyetoroka wakati Yahwe akiwaongoza watu wa Israeli kupita nchi kavu. "Ni kana kwamba bahari lilitazama na kutoroka"

Yordani ikageuka

Mwandishi anazungumzia mto Yordani kana kwamba ni mtu aliyerudi nyuma wakati Yahwe akiwaongoza watu wa Israeli kwenye nchi kavu. "ilikuwa kana kwamba Yordani ilirudi"

Milima ikaruka kama kondoo dume, vilima vikaruka kama wanakondoo

Mwandishi anazungumzia milima na vilima kana kwamba zilikuwa hai. Inawezekana anazungumzia tetemeko anapoelezea uoga wao kwenye uwepo wa Yahwe jinsi wanavyoruka kama kondoo dume na wanakondoo. "Ilikuwa kana kwamba milima ilitikisika kama kondoo dume wanaoruka na vilima vilitikisika kana kwamba wanakondoo wanavyoruka.

Psalms 114:5

Taarifa ya Jumla:

Mistari ya 5-6 ina maswali manne ya balagha. Jibu linalotarajiwa kwa kila swali linapatikana katika mstari wa 7, "kwa sababu ya uwepo wa Bwana."

uliruka kama kondoo dume ...uliruka kama wanakondoo

Mwandishi anazungumzia milima na vilima kana kwamba zilikuwa hai. Inawezekana anazungumzia tetemeko anapoelezea uoga wao kwenye uwepo wa Yahwe jinsi wanavyoruka kama kondoo dume na wanakondoo. "Ilikuwa kana kwamba milima ilitikisika kama kondoo dume wanaoruka na vilima vilitikisika kana kwamba wanakondoo wanavyoruka.

Tetemeka dunia, mbele ya Bwana, kwenye uwepo wa Mungu wa Yakobo

Misemo miwili ya mwisho ina usambamba. Kitenzi kinaweza kuwekwa kwenye mstari wa pili. "Tetemeka dunia, mbele ya Bwana, tetemeka mbele ya uwepo wa Mungu wa Yakobo"

Tetemeka dunia

Maana zinazowezekana ni 1) mwandishi anazungumzia dunia kana kwamba ni mtu na anaiamuru kutetemeka kwa uoga mbele za Mungu au 2) neno "dunia" ni njia nyingine ya kusema wale wanaoishi duniani. "Tetemekeni, watu wote duniani"

Psalms 114:8

Akageuza jiwe kuwa bwawa la maji, jiwe gumu kuwa chechemi ya maji

Misemo hii mwili ina usambamba. Mwandishi anamuelezea Yahwe kusababisha maji kutiririka kutoka kwenye jiwe kana kwamba aliligeuza jiwe kuwa maji.

mwamba mgumu kuwa chechemi ya maji

Kitenzi kinaweza kutolewa kuwekwa kwenye msemo uliopita. "Akageuza jiwe gumu kuwa chemchemi ya maji"

Psalms 115

Psalms 115:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Sio kwetu, Yahwe, sio kwetu

Mwandishi anarudia msemo "sio kwetu" ili kusisitiza kwamba hawastahili kupokea heshima anayostahili Yahwe pekee. "Usilete heshima kwetu, Yahwe"

kwetu

Neno "kwetu" linamaanisha watu wa Israeli.

lakini kwa jina lako leta utukufu

Hapa neno "jina" linaashiria Yahwe mwenyewe. "lakini leta utukufu kwako mwenyewe"

kwa ajili ya uaminifu wako wa agano

"kwa sababu ya uaminifu wako wa agano"

Kwa nini mataifa yaseme, "Yuko wapi Mungu wao?"

Hili swali la balagha linasisitiza kuwa hakuna sababu ya mataifa kusema wanayosema. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Watu wa mataifa hawatakiwa kuwa na uwezo wa kusema, 'Yuko wapi Munguwao?'"

Yuko wapi Mungu wao?

Watu wa mataifa mengine wanatumia swali hili kuwadhihaki watu wa Israeli na kuonesha kuwa hawaoni Yahwe akiwasaidia. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Mungu wenu hayupo hapa kuwasaidia"

Psalms 115:3

kazi ya mikono ya watu

Hapa neno "mikono" inaashiria watu waliotengeneza hizo sanamu. "vitu ambavyo watu wametengeneza"

Psalms 115:5

Hizo sanamu zina midomo

Sanamu hazina midomo ya kweli, macho, maskio, au pua za kweli. Lakini, watu wamewaunda na mifano ya midomo, macho, maskio, na pua. Mwandishi anasisitiza kuwa sanamu haziko hai kweli. "Watu wamezipa midomo hizo sanamu"

Psalms 115:7

Hizo sanamu zina midomo

Sanamu hazina midomo ya kweli, macho, maskio, au pua za kweli. Lakini, watu wamewaunda na mifano ya midomo, macho, maskio, na pua. Mwandishi anasisitiza kuwa sanamu haziko hai kweli. "Watu wamezipa midomo hizo sanamu"

lakini hawahisi

"lakini mikono hio haihisi"

Wale wanaozitengeneza ni kama hizo sanamu, kama alivyo kila mtu anayezitegemea

Wale wanaounda na kuabudu sanamu wanakuwa bila uhai na wasio na nguvu , kama hizo sanamu. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "Wale wanaozitengeneza wanakosa uhai kama hizo sanamu, kama watu wengine wote wanaozitumaini"

Psalms 115:9

Israeli, mtumainini Yahwe

Neno "Israeli" linaashiria watu wa Israeli. "watu wa Israeli, mtumainini Yahwe"

msaada wenu na ngao

Mwandishi anamzungumzia Yahwe kana kwamba ni ngao kwa sababu anawalinda watu wake kama ngao inavyowalinda kutokana na madhara. "yule ambaye anawasaidia na kuwalinda"

Nyumba ya Haruni

Hapa neno "nyumba" linamaanisha familia au uzao. Msemo huu unamaanisha makuhani, walikuwa uzao wa Haruni. "Uzao wa Haruni" au "Makuhani"

Psalms 115:12

tuangali

"ametuangalia kwa makini"

familia ya Israeli

Hii inamaanisha watu wa Israeli, ambao ni uzao wa Yakobo, ambaye pia aliitwa Israeli. "watu wa Israeli"

familia ya Haruni

Hii inamaanisha makuhani, ambao ni uzao wa Haruni. "Uzao wa Haruni" au "Makuhani"

wote wachanga na wazee

"wote wadogo na wakubwa." Maana zinazowezekana ni kwamba hii inaashiria 1) hadhi katika jamii au 2) umri. Vyovyote vile, tofauti hizi mbili zinawakilisha kila mtu, bila kujali umri au hadhi katika jamii.

Na Yahwe aongeze idadi yenu zaidi na zaidi

Mwandishi anazungumzia idadi ya watoto ambayo watu wa Israeli watakuwa nayo. "Na Yahwe awazidishie idadi ya watoto wenu zaidi na zaidi"

yenu na ya uzao wenu

"wote watoto wenu na uzao wa watoto wenu." Mwandishi anaweka wazi kuwa ombi lake kwa ajili ya watoto zaidi halimaansihi kizazi cha sasa tu bali kwa uzao wao pia.

Psalms 115:15

Na mbarikiwe na Yahwe, aliyeumba mbingu na nchi

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Na Yahwe, aliyeumba mbingu na nchi, awabariki"

dunia amempa mwanadamu

Hii haimaanishi kuwa dunia si mali ya Yahwe, lakini amewapa binadamu dunia kama sehemu ya makao.

Psalms 115:17

Wafu

Kivumishi "wafu" kinaweza kutafsiriwa na msemo wa nomino. "Watu waliokufa"

wala yeyote anayeenda chini palipo nyamaza

Msemo huu wa usambamba unamaana sawa na msemo uliopita. Kitenzi kinaweza kuwekwa kutoka kwenye msemo uliopita kuweka maana yake wazi. "wala yeyote aendaye chini palipo nyamaza kumsifu Yahwe"

wala yeyote anayeenda chini kunyamaza

Mwandishi anazungumzia kaburi au sehemu ya wafu kama sehemu iliyo nyamaza ambapo hakuna awezaye kuzungumza. Hii ni tasifida ya kifo. "wala yeyote anayeenda sehemu ya wafu"

Lakini sisi

Neno "sisi" linamaanisha watu wa Israeli walio hai bado.

Psalms 116

Psalms 116:1

Taarifa ya jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

husikia saauti yangu na maombi yangu ya huruma

Hapa neno"sauti" linawakilisha mtu anayeongea. Msemo, "maombi yangu ya huruma" unaeleza anachokisema. "hunisikia ninapojieleza kwa ajili ya huruma"

Psalms 116:3

Taaarifa ya Jumla:

Mtu aliyetunga zaburi hii anaendelea kuzungumza.

Kamba za kifo zilinizunguka

Mwandishi anazungumzia kifo kanakwambani mtu anayeweza kumshika na kumfunga kwa kamba. "Nilihisa kama nataka kufa"

mitego ya kuzimu ilinikabili

Mwandishi anazungumzia "kuzimu," mahali pa wafu, kana kwambani mtu anayeweza kumtega kwamitego. "Nilihisi kama niko tayari kuingia kaburini"

nikalita jina la Yahwe

Hapa neno "jina" linaashiria Yahwe mwenyewe. "nikamwita Yahwe"

okoa maisha yangu

Hapa neno "maisha" linaashiria mtu. "niokoe" au "niepushe na kufa"

Psalms 116:5

Taarifa ya Jumla:

Mtu aliyetengeneza wimbo huu anaendelea kuzungumza.

wasio na hila

Hii inamaanisha watu wasikuwa na uzoefu au hawawezi kujitunza. Kivumizhi kinaweza kutafsiriwa kama msemo wanomino. "wale wasio na hila" au "wale wasiojiweza"

nililetwa chini

Mwandishi anazungumzia kunyenyekeshwa kama kuwa nafasi ya chini zaidi. "Nilikuwa sijiwezi"

Psalms 116:7

Taarifa ya Jumla:

Mtu aliyetunga zaburi hii anaendelea kuzungumza.

Nafsi yangu inaweza kurudi sehemu yake ya kupumzika

Mwandishi anazungumzia kuwa na amani na ujasiri kana kwamba ilikuwa ni sehemu ambapo nafsi yake ingeweza kupumzika. Neno "nafsi" linawakilisha mtu. "Ninaweza kupumzika kwa amani tena"

uliokoa maisha yangu na kifo

Aliyemwokoa ni Yahwe. Neno "maisha" yanaashiria mtu. "umeniokoa na kifo" au "umeniepusha na kifo"

macho yangu na machozi

Msemo wa kitenzi unawaweza kuwekwa kutoka msemo uliopita kuweka maana wazi. "umeokoa macho yangu na machozi" au "umeniepusha na kulia"

miguu yangu na kuanguka

Msemo wa kitenzi unawaweza kuwekwa kutoka msemo uliopita kuweka maana wazi. Miguu hapa inaashiria mtu. Kuanguka hapa inaweza kuwa inamaanisha kuuliwa na adui zake. "umeniokoa na kuanguka" au "umeniepusha na kuuliwa na adui zangu"

Psalms 116:9

Taarifa ya Jumla:

Mtu aliyetunga zaburi hii anaendelea kuzungumza.

katika nchi ya walio hai

"kwenye dunia hii ambapo watu wako hai." Hii ni tofauti na sehemu ya wafu.

Nimeumizwa sana

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Ninahangaika sana" au "Watu wananiumiza sana"

Nikasema haraka

"Nikasema haraka sana" au "Nikasema bila kutafakari"

Wanaume wote ni waongo

"Kila mtu ni muongo" au "Watu wote ni waongo"

Psalms 116:12

Taarifa ya Jumla:

Mtu aliyetengeneza wimbo huu anaendelea kuzungumza.

Nitamlipaje Yahwe ... kwangu?

Mwandishi anauliza swali hili kutambulisha jinsi atakavyojibu kwa yale Yahwe aliyofanya. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Hivi ndivyo nitakavyomlipa Yahwe ... kwangu."

Nitainua kikombe cha wokovu

Hii inawezekana kuwa marejeo ya kinywaji, ambayo ilikuwa ni sadaka iliyohusisha kumwaga divai katika madhabahu, na ambayo mwandishi atatoa kwa Yahwe kwa kumwokoa. "Nitatoa sadaka ya kinywaji kwa yahwe kwa kuwa ameniokoa"

kuliita jina la Yahwe

Hap neno "jina" limwakilisha Yahwe mwenyewe. "kumwita Yahwe"

Ya thamani machoni pa Yahwe mauti ya watakatifu wake

Neno "thamani" hapa haimaanishi kuwa Yahwe anathamini vifo vya watakatifu wake, lakini vifo vya watakatifu wake vinamgharimu na kumhuzunisha. Msemo "machoni pa" inawakilisha moyo wa Yahwe kwenye kitu anachokiona. "Yahwe anaona kuwa vifo vya watakatifu wake ni jambo la gharama"

Psalms 116:16

Taarifa ya Jumla:

Mtu aliyetunga zaburi hii anaendelea kuzungumza.

mwana wa mtumishi wako mwanamke

Hii inawezekana kuwa mrejeo wa mama yake mwandishi na inaashiria kuwa alimwabudu Yahwe kwa uaminifu. Maana kamili inaweza kuwekwa wazi. "kama mama yangu alivyokuwa"

umenitolea pingu zangu

Mwandishi anazungumzia kuwa hatarini kufa kana kwamba alikuwa amefungwa gerezani."umeniokoa na kifo"

sadaka ya shukrani

"sadaka kuonesha shukrani yangu"

kuliita jina la Yahwe

Hapa neno "jina" linamwakilisha Yahwe mwenyewe. "kumwita Yahwe"

Psalms 116:18

Taarifa ya Jumla:

Mtu aliyeandika wimbo huu anaendelea kuzungumza.

Nitatimiza ... watu wake wote

"Nitatimiza nadhiri zangu kwa Yahwe ili watu wote waone"

katika baraza la nyumba ya Yahwe

Neno "nyumba" linamaanisha hekalu ya Yahwe. "katika baraza la hekalu ya Yahwe"

katikati yako, Yerusalemu

Mwandishi anazungumza na Yerusalemu kana kwamba anazungumza na mtu. "katika Yerusalemu"

Psalms 117

Psalms 117:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa

"Kwa sababu"

uaminifu wake wa agano ni mkubwa kwetu

"uaminifu wake wa agano kwetu ni mkubwa "

unadumu milele

"upo milele"

Psalms 118

Psalms 118:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Mpeni Yahwe shukrani, kwa kuwa ni mwema

"Mshukuruni Yahwe kwa mambo mema ambayo huwa anafanya"

Uaminifu wake wa agano unadumu milele

"Anatupenda kwa uaminifu milele"

Acha israeli iseme

Neno "Israeli" linawakilisha watu wa Israeli. "Acha watu wa Israeli waseme"

Psalms 118:3

Acha nyumba ya Haruni iseme

Hapa neno "nyumba" linawakilisha familia na uzao wa mtu. Msemo huu unamaanisha makuhani, ambao walikuwa uzao wa Haruni. "Acha uzao wa Haruni useme" au "Acha makuhani waseme"

Uaminifu wake wa agano unadumu milele

"Anatupenda kwa uaminifu milele"

wafuasi waaminifu wa Yahwe

"wale wanaomcha Yahwe" au "wale wanaomwabudu Yahwe"

Psalms 118:5

akaniweka huru

Mwandishi anazungumzia Yahwe kumwokoa kutoka kwenye huzuni kana kwamba Yahwe alimtoa kutoka sehemu ya kifungo hadi sehemu pana ya wazi ambapo angeweza kusogea kwa uhuru.

mtu atanifanya nini?

Mwandishi anauliza swali hili balagha kusisitiza kuwa hakuna kitu ambacho mtu anaweza kufanya kumuumiza kwa kuwa Yahwe yuko pamoja naye. "watu hawawezi kufanya chochote kunidhuru"

Yahwe yuko upande wangu kama msaidizi wangu

Kuwa upande wa mtu ni lahaja inayoashiria kuwa mtu anakubaliana na atamsaidia mtu mwingine. "Yahwe ananikubali na atanisaidia"

nitatazama kwa ushindi juu ya wale wanaonichukia

Inadokezwa kuwa Yahwe ndiye atakayewashinda adui wa mwandishi, wakati mwandishi akitazama. "Nitamwona Yahwe akiwashinde wote wanaonichukia"

Psalms 118:8

kujihifadhi kwa Yahwe

Mungu anazungumziwa kana kwamba ni kivuli, sehemu ambayo watu wanaweza kulindwa. "kutafuta ulinzi kutoka kwa Yahwe"

kumkimbilia Yahwe

Mstari huu una usambamba na ule uliopita. Mungu anazungumziwa kana kwamba ni kimbilio, sehemu ambayo watu wanaweza kulindwa. "kutafuta ulinzi kutoka kwa Yahwe"

Psalms 118:10

Mataifa yote

Hapa neno "mataifa" inawakilisha majeshi ya mataifa hayo. Mwandishi anatumi kukuza kwa neno kusisitiza idadi kubwa ya majeshi yaliyomzunguka. "Majeshi ya mataifa mengi"

katika jina la Yahwe

Hapa neno "jina" linawakilisha nguvu ya Yahwe. "kwa nguvu ya Yahwe"

ninawakata

Mwandishi anazungumzia kuyashinda majeshi ya adui kana kwamba alikuwa akiyakata kama mtu anavyokata tawi kwenye mmea. "niliwashinda"

wananizunguka kama nyuki

Mwandishi analinganisha majeshi ya adui na kundi kubwa la nyuki yatamzunguka mtu"

walipotea haraka kama moto kwenye miiba

Kama miiba iliyokauka inavyowaka upesi, mashambulizi ya majeshi ya adui yaliisha ghafla. "mashambulizi yao yalidumu kwa muda mfupi, kama moto unaoteketeza miiba unavyoisha upesi"

Psalms 118:13

kuniangusha chini

Mwandishi anazungumzia majeshi ya adui kujaribu kumshinda kana kwamba walikuwa wakijaribu kumsukuma ardhini. "ili kunishinda mimi"

Yahwe ni nguvu yangu na furaha yangu

"Yahwe hunipa nguvu na furaha"

Psalms 118:15

Sauti ya kelele ya ushindi inasikika katika mahema ya wenye haki

"Watu husikia kelele ya furaha katika mahema ya wenye haki" au "Wenye haki wanapiga kelele kwa furaha ya ushindi kwenye mahema yao"

mkono wa kuume wa Mungu unashinda

Hapa neno "mkono" linawakilishi uwezo wa Yahwe. "Yahwe ameshinda kwa nguvu yake kuu"

mkono wa kuume wa Mungu unashinda

Hapa, kuinua mkono ni ishara ya ushindi. "Yahwe ameinua mkono wake wa kuume" au "Yahwe ameinua mkono wake wa kuume kwa ushindi"

Psalms 118:17

Sitakufa, bali nitaishi

Mwandishi anaeleza wazo moja kwa njia hasi na chanya kusisitiza kuwa hakika ataishi.

Yahwe ameniadhibu

"Yahwe amenifundisha"

hajanikabidhi kwa mauti

Mwandishi anazungumzia mauti kana kwamba ni mtu ambaye Yahwe anaweza kumweka mtu chini ya uwezo wake. "hajaniruhusu kufa" au "hajawaruhusu adui zangu kuniua"

Psalms 118:19

Nifungulie malango ya haki

Nifungulie malango ambayo watu wenye haki hupita." Hii inamaanisha malango ya hekalu, na mwandishi anawaambia walinzi wa malango. "Nifungulieni malango ya hekalu"

lango la Yahwe

"lango unaowaongoza watu kuelekea katika uwepo wa Yahwe " au "lango la Yahwe"

nitatoa shukrani kwako

Hapa mwandishi anaanza kuzungumza na Yahwe.

umekuwa wokovu wangu

"uliniokoa"

Psalms 118:22

Jiwe ambalo wajensi walikataa limekuwa jiwe kuu la pembeni

Hii inaweka kuwa mithali ambayo mwandishi ametumia kuelezea mojawapo kati ya mfalme ya taifa la Israeli. Lile ambalo watu wameona halifai, Yahwe amelifanya kuwa la muhimu zaidi.

ni la ajabu machoni petu

Maana zinazowezekana ni 1) "ni jambo la ajabu kwetu kuona" au 2) "tunaona kuwa jambo la ajabu ."

Psalms 118:24

tutashangilia na kufurahi

Misemo hii inamaana moja na inasisitiza uzito wa furaha. "tutashangilia sana"

Psalms 118:26

Amebarikiwa anayekuja kwa jina la Yahwe

Hapa makuhani wanaanza kuzungumza na mfalme.

anayekuja kwa jina la Yahwe

Hapa neno "jina" linawakilisha uwezo wa Yahwe. "yule anayekuja katika nguvu ya Yahwe"

tutakubariki kutoka katika nyumba ya Yahwe

Hapa makuhani wanazungumza na watu.

nyumba ya Yahwe

Neno "nyumba" linamaanisha hekalu. "hekalu la Yahwe"

ametupa nuru

Mwandishi anamzungumzia Yahwe kuwabariki watu wake kana kwamba Yahwe anamulika mwanga juu yao. "ametubariki"

funga sadaka kwa kamba

"kaza sadaka kwa kamba"

Wewe ni Mungu wangu

Hapa mwandishi anaanza kuzungumza tena na anazungumza na Yahwe moja kwa moja.

Psalms 118:29

O

Huu ni mshangao.

mpeni Yahwe shukrani; kwa kuwa ni mwema

"Mshukuruni Yahwe kwa mambo mema ambayo huwa anafanya"

uaminifu wake wa aganounadumu milele

"anatupenda kwa uaminifu milele."

Psalms 119

Psalms 119:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

ALEFU

Hili ni jina la herufi ya kwanza ya alfabeti ya Kihebrania.

Wamebarikiwa wale

"Ni vizuri vikoje kwa wale"

wale ambao njia zao hazina lawama

Jinsi mtu anavyotenda inazungumziwa kama "njia." "wale ambao tabia zao hazina lawama" au "wale ambao hakuna anayeweza kuwalaumu kwa kutenda makosa"

wanao tembea katika sheria ya Yahwe

Jinsi mtu anavyoishi au kutenda inazungumziwa kama kutembea. "wanaoishi kulingna na sheria ya Yahwe" au "wanaotii sheria ya Yahwe." Msemo huu unaweka wazi maana ya "ambao njia zao hazina lawama."

wanaomtafuta kwa moyo wao wote

"Kumtafuta" Mungu inamaanisha kutaka kumjua.

kwa moyo wao wote

Hii ni lahaja inayomaanisha kwa nguvu au kwa ukweli. "kwa hali yao yote" au "kwa kila kitu ndani yao" au "kwa kweli"

Psalms 119:3

Taarifa ya Jumla:

Sehemu kubwa ya zaburi hii inaelekezwa kwa Mungu, na maneno "wewe" na "zako" mara nyingi zinamaanisha yeye.

Hawafanyi kosa

Hawamkaidi Yahwe

wanatembea katika njia zake

"wanatembea katika njia za Yahwe." Hapa tabia yao inazungumziwa kama "kutembea," na jinsi Mungu anavyoteka waenende inazungumziwa kama "njia zake." "wanaenenda kama Yahwe anavyotaka waenende"

kutunza maagizo wako

"kutii vitu vyote ambavyo umesema tunapaswa kufanya"

tuziangalie kwa uangalifu

Hii ni kujua kwa umakni na kuelewa amri na kuzitii hizo amri.

Psalms 119:5

nitawekwa thabiti

Mwandishi anazungumzia kuimarishwa katika amri za Mungu kana kwamba hakuna mtu anayeweza kumsogeza kimwili.

kuangalia sheria zako

"katika kutii sheria zako"

sitaaibishwa

Mwandishi hataki kuaibishwa akiwa katika uwepo wa Mungu.

amri zako zote

"yote uliyo tuamuru"

Psalms 119:7

moyomnyofu

"moyo wa ukweli." Mtu ambaye ni mkweli atafanya kilicho sawa. Moyo unamaanisha kiini cha hisia ndani ya mtu.

sheria zako

"Sheria" inamaanisha sheria au amri za Mungu.

Psalms 119:9

BETH

Hili ni jina la herufi ya pili ya alfabeti ya Kihebrania. Katika lugha ya Kihebrabia, kila mstari katika mistari ya 9-16 unaanza na herufi hii.

Kijana atasafishaje njia yake?

Swali hili linatumika kutambulisha faida mpya katika neno la Mungu. Swali hili balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Hivi ndivyo kijana anavyoweza kusafisha njia yake"

atasafishaje njia zake

Mwandishi anafananisha kuishi kulingana na sheria ya Mungu kama njia unayowekwa wazi bila vikwazo.

Kwa moyo wangu wote

Hii ni lahaja. Moyo unawakilishi hisia, hamu, na mapenzi ya mtu. "kwa hali yangu yote" au "kwa kila kitu ndani yangu" au "kwa ukweli"

Usiniache nipotea kutoka katika amri zako

Hapa kutotii amri za Mungu inaelezwa kama kupotoka njia. "Usiniache nikaidi amri zako"

Psalms 119:11

Nimetunza neno lako moyoni mwangu

"Nimeweka maneno yako moyoni mwangu." Hii ni sitiari inayomaanisha "Nimekalili neno lako." Moyo unaoneshwa kama chombo kinachoweza kutunza kile ambacho watu wanafikiri.

Psalms 119:13

zaidi ya utajiri wote

"zaidi ya mali zote"

Psalms 119:15

Nitatafakari ... na kuzingatia

Haya ni mawazo ya usambamba yenye maana ya kufanana, zinazotenganishwa kwa ajili ya mkazo.

Nitatafakari maagizo yako

"kuwaza kwa umakini kuhusu ulichotuelekeza"

kuzingatia

Lahaja hii inamaanisha kuwaza vizuri kuhusu kinachojadiliwa. "kuwaza kwa makini"

Nafurahi

kufurahi katika

Psalms 119:17

GIMELI

Hili ni jina la herufi ya tatu ya alfabeti ya Kihebrabia. Katika lugha ya Kihebrania, kila mstari wa mistari ya 17-24 unaanza na herufi hii.

mtumishi wako

Mwandishi alijiita "mtumishi wako" kuonesha unyenyekevu.

Fungua macho yangu ili nione

Mwandishi anazungumzia kupata uelewa, maarifa na hekima kama kuweza kuona. "Nisaidie nielewe"

mambo ya ajabu katika sheria yako

Mwandishi anazungumzia utambuzi wa sheria kama vitu vya kustaajabu.

katika sheria yako

"katika maagizo yako" au "katika amri zako"

Psalms 119:19

Mimi ni mgeni katika nchi

Maana zinazowezekana ni 1) mwandishi anazungumzia maisha yake mafupi duniani kana kwamba ni mgeni ambaye hatakuwa katika nchi kwa muda mrefu. "Mimi ni kama mgeni anayeishi kwa mudamfupi katika nchi" au 2) ujinga wa mwandishi wa sheria ya Mungu ni kana kwamba alikuwa mgeni ambaye hakuwa anajua sheria za nchi. "Sijui kama mgeni katika nchi"

Hamu zangu zinapondwa kwa shauku

Mwandishi anazungumzia hamu yake ya kuwa imara kama alikuwa katika maumivu. "Hali yangu ya ndani inatamani sana kukujua" au "Nafsi yangu inaumia kwa sababu nataka sana kujua"

Psalms 119:21

waliolaaniwa

Maana zinazowezekana ni 1) Mungu atawalaani au 2) wanastahili adhabu ya Mungu. "wanaostahili adhabu yako"

wanaopotea kutoka katika amri zako

Mwandishi anazungumzia kutotii amri za Mungu kana kwamba zilikuwa ni njia ambayo mtu anaweza kupotoka. "wanaoenda mbali na njia za amri zako" au "wanaokaidi amri zako"

Niepushe na

"Niweke mbali na" au "Niokoe na"

na aibu

"na kuhisi aibu na upumbavu"

Psalms 119:23

Ingawa watawala wanapanga hila na kunikashifu

"Ingawa watawala hufanya mipango ya kunidhuru na kusema vitu vibaya kunihusu"

Amri zako za agano ni furaha yangu

"Amri zako za agano zinanifanya kuwa na furaha sana"

na ni ushauri wangu

Amri za Mungu zinazungumziwa kana kwamba ni watu. "na ni kama washauri wenye hekima kwangu" au "na wananipa ushauri wa hekima"

Psalms 119:25

DALETI

Hili ni jina la herufi ya nne ya alfabeti ya Kihebrania. Katika lugha ya Kihebrabia, kila mstari wa msistari ya 25-32 unaanza na herufi hii.

Maisha yangu yanang'ang'ania kwenye mavumbi

Hii ni lahaja. Maana zinazowezekana ni kwamba 1) alidhani kuwa atakufa punde, au 2) alilala kwenye mavumbi kwa sababu alikuwa na huzuni sana, au 3) aligundua kuwa alitamani vitu visivyo na faida vya duniani.

Nipe maisha kwa neno lako

Hii ni lahaja. Hapa "maisha" inamaanisha kusudi na umuhimu, sio maisha ya kimwili tu.

kwa neno lako

"Neno" la Mungu linawakilisha alichokisema. Hapa linamaanisha alichoahidi. "kulingana na ahadi yako"

njia zangu

Kile ambacho mtu hufanya au jinsi anavyoenenda inazungumziwa kana kwamba ni barabara au njia. "nilichofanya"

Psalms 119:27

mafunzo ya ajabu

"mafunzo ya kushangaza"

kwa huzuni

"kwa sababu nina huzuni"

Nime nguvu

"Nifanye kuwa imara." Hii inaweza kumaanisha nguvu ya kimwili au nguvu ya kiroho.

Psalms 119:29

Nigeuze kutoka katika njia ya udanganyifu

Neno "njia" hapa linamaanisha namna ya kuenenda kitabia. "Niepushe na kufuata njia ya udanganyifu" au "Niepushe kutokuwa mdanganyifu"

udanganyifu

Maana zinazowezekana ni 1) kudanganya" au 2) "kuamini uongo" au "kufuata uongo"

njia ya uaminifu

Jinsi mtu anavyoenenda kitabia au kutenda inazungumziwa kana kwamba ni barabara au njia. "kuwa mwaminifu kwako"

Psalms 119:31

Nashilia amri zako za agano

Kuzishikilia kwa nguvu inamaanisha kuwa na nia ya kuzitii. "Ninashikilia kwa nguvu amri zako za agano" au "Nina nia ya kutii amri zako za agano"

amri za agano

Hii inamaanisha sheria za Musa.

Nitakimbia katika njia ya amri zako

Mwandishi anazungumzia kuwa makini au kuwa na nia ya kutii amri za Mungu kana kwamba mtu anakimbia katika njia. "Nitakuwa na nia ya kutii amri zako"

unaukuza moyo wangu

Hii ni lahaja. Maana zinazowezekana ni 1) "unanisaidia kupata uelewa mkubwa wa amri zako"

Psalms 119:33

HE

Hili ni jina la herufi ya tano ya alfabeti ya Kihebrania. Katika lugha ya Kihebrabia, kila mstari wa msistari ya 33-40 unaanza na herufi hii.

sheria zako

Hii ni njia nyingine ya kueleza sheria ya Musa.

hadi mwisho

Maana zinazowezekana ni 1) "kabisa" au 2) "hadi mwisho wa maisha yangu" au 3) "hadi mwisho wa wakati"

nitatunza sheria yako

"kutii sheria yako"

nitaiangalia kwa moyo wangu wote

"Hakika nitaifuata sheria yako" au "Nina nia kabisa ya kufanya isemacho"

kwa moyo wangu wote

Hii ni lahaja. "kwa hali yangu yote" au "kwa kila kitu ndani yangu" au "ki ukweli"

Psalms 119:35

Niongoze katika njia ya amri zako

"Niongoze kulingana na amri zako" au "Nifundishe kutii amri zako." Amri za Mungu zinalinganishwa na njia ambayo mtu anatembea akimtii Mungu.

Ongoza moyo wangu kuelekea

Hii ni lahaja. "Moyo" hapaunamaanisha nia, hamu, na maamuzi yanayoongoza maisha ya mtu. "Unifanye nitake"

amri zako za agano

"kutii amri zako za agano." Hii inamaanisha kutii amri za Musa.

kuongezeka pasipo haki

"hamu ya utajiri." Hii inamaanisha utajiri unaopatikana kwa njia zisizo sawa au kuwatendea ubaya wengine.

Psalms 119:37

Geuza macho yangu yasitazame vitu visivyo na faida

Hii ni sitiari inayomaanisha mtu anayetamani vitu ambavyo havina thamani ya milele.

nifufue katika njia zako

"nifanye niweze kuishi kama unavyotaka niishi"

nifufue

"fanya maisha yangu yawe imara" au "nipe nguvu"

Tekeleza kwa mtumishi wako ahadi yako uliyoahidi wale wanao kuheshimu

"Fanya kwa mtumishi wako kile ulichoahidi kufanya kwa wale wanao kuheshimu"

mtumishi wako

Mwandishi anajieleza kama mtumishi wa Mungu kuonesha unyenyekevu. "mimi, mtumishi wako"

Psalms 119:39

ninayo hofu

"ninaogopa sana"

hukumu zako za haki ni nzuri

Mungu anahukumu kwa haki na maamuzi yake ni mema. "Hukumu yako ni ya haki na njema"

Tazama

Hii ni lahaja. Hapa "Tazama" inamaanisha kuwa na ufahamu kuhusu jambo. Panapo lengwa ni maarifa na uelewa, na sio tu kutazama.

Nina shauku na maagizo yako

Maana zinazowezekana ni 1) "Ninataka sana kujua maagizo yako" au 2) "Ninataka sana kutii kile unachotufundisha kufanya"

nifufue katika haki yako

Neno "haki" ni nomino dhahania na inamaanisha kuwa mwenye haki. "nifufue kwa kuwa una haki"

nifufue

Maana zinazowezekana ni 1) "Niweke kuwa hai" au 2) "Nifanye kuwa na nguvu"

Psalms 119:41

VAV

Hili ni jina la herufi ya sita ya alfabeti ya Kihebrania. Katika lugha ya Kihebrabia, kila mstari wa msistari ya 41-48 unaanza na herufi hii.

nipe upendo wako usiokoma

Hili ni ombi. "tafadhali nipe upendo wako usiokoma"

wokovu wako

"nipe wokovu wako" au "niokoe"

jibu

"itikio"

Psalms 119:43

Usitoe neno la ukweli mdomoni mwangu

"mdomo wangu" inamaanisha kuzungumzia juu ya neno la Mungu. "Usinizuie kamwe kuzungumza ukweli wako"

kwa kuwa nimesubiri amri zako za haki

"kusubiri" kuna wazo la kuamini, kuwa na uhakika kuwa Mungu atafanya anavyoagiza.

Nitafuata

"Nitatii"

Psalms 119:45

NItatembea salama

Kutembea salama ni kuishi maisha kwa usalama. "Nitaishi kwa usalama katika Mungu"

natafuta maagizo yako

"Kutafuta" ni kutambua, au kupata uelewa wa maagizo ya Mungu kana kwamba mtu anaweza kuyaona.

amri zako makini mbele ya wafalme

"amri za dhati kwa wafalme" au "maagizo kwa wafalme"

Psalms 119:47

Ninafurahi katika amri zako

Maana zinazowezekana ni 1) "Ninapata furaha katika kusoma amri zako" au 2) "Ninafuraha kuwa nina nafasi ya kusoma amri zako"

nitainua mikono yangu

Hii ni lahaja inayomaanisha kutunza au kuheshimu amri za mungu.

Psalms 119:49

ZAYINI

Hili ni jina la herufi ya saba ya alfabeti ya Kihebrania. Katika lugha ya Kihebrabia, kila mstari wa msistari ya 49-56 unaanza na herufi hii.

Itisha akilini ahadi yako

"Kumbuka ahadi yako."

Hii nifaraja yangu katika mateso; kuwa ahadi yako imeniweka hai

"Sababu ya faraja yangu ni kwamba ahadi yako imeniweka hai katika mateso yangu"

Psalms 119:51

Wenye kiburi

"Watu wenye kiburi"

wamenikejeli

kumdhihaki mtu au kitu kinachodharauliwa, chenye wasiwasi, au kischo heshimiwa

za nyakati za zamani

Huu ni mrejeo kwa kipindi sheria zimepewa kwa Musa miaka mingi kabla.

Psalms 119:53

Hasira ya moto imenishika

Hii ni lahaja. Hasira inaelezwa kana kwamba ni mtu anayeweza kumkamata mtu mwingine. "Nimekuwa na hasira sana"

Sheria zako zimekuwa nyimbo zangu

"Nimetumia sheria zako kama maneno ya muziki wangu" au "Nimutunga nyimbo kutokana na sheria zako"

Psalms 119:55

Nafikiria kuhusu jina lako

Hapa neno "jina" linamwakilisha Yahwe mwenyewe. "Nakuwaza, Yahwe"

natunza sheria yako

Hii ni lahaja inayomaanisha kutii sheria. "Ninatii sheria yako"

zoezi langu

"tabia yangu"

nimefuata maagizo yako

"Nimetii maagizo yako"

Psalms 119:57

HETHI

Hili ni jina la herufi ya nane ya alfabeti ya Kihebrania. Katika lugha ya Kihebrabia, kila mstari wa msistari ya 57-64 unaanza na herufi hii.

Yahwe ni sehemu yangu

Hii inamaana kuwa Yahwe ndio kitu pekee anachotaka. Kama ambavyo Walawi hawapati maeneo makubwa ya nchi kwa kuwa Bwna ndiye alipaswa kuwa sehemu yao, kwa hiyo mwandishi anatamka kuwa Yahwe ni anayerithisha hamu zake.

Psalms 119:59

nikageuza miguu yangu

Hapa "miguu" inamwakilisha mtu mzima. Kutubu na kuchagua kutii sheria za Mungu ni kama kugeuza miguu kwenye njia na kuelekea upande mwingine. "nilibadilisha mwelekeo"

Ninaharakisha na sichelewi

Mwandishi anaeleza wazo moja katika hali chanya na hasi ili kusisitiza uharaka alionao katika kutii amri za Yahwe.

Psalms 119:61

Kamba za waovu zimeninasa

Katika sitiari hii, watu waovu walijaribu kumfanya mwandishi kutenda dhambi kama mwindaji anavyotafuta kumnasa mnyama kwa mtego. "Adui zangu wamejaribu kunishika"

Psalms 119:63

Mimi ni mwenzao wale wote waokuheshimu

"Mimi ni rafiki wa wale wote waokuheshimu"

Psalms 119:65

TETHI

Hili ni jina la herufi ya tisa ya alfabeti ya Kihebrania. Katika lugha ya Kihebrabia, kila mstari wa msistari ya 65-72 unaanza na herufi hii.

kwa mtumishi wako

Mwandishi anajieleza kama "mtumishi wako." "kwangu, mtumishi wako" au "kwangu"

kwa njia ya neno lako

Hii ni lahaja. "Neno lako" inamaanisha ahadi za Yahwe alizompa mwandishi. "kama ulivyoahidi"

Psalms 119:67

Kabla sijateseke

"Kabla haujanitesa" au "Kabla haujaniadhibu"

nilipotoka

Kumkaidi Mungu inazungumziwa kana kwamba mtu anatembea katika njia isiyofaa. "Sikukutii wewe"

ninafuata neno lako

Hapa "neno" linawakilisha amri. "ninatii amri zako"

Psalms 119:69

Wenye kiburi

"Watu wenye kiburi"

walinipaka na uongo

Watu kusema uongo kuhusu mtu inazungumziwa kana kwamba wamemfanya mtu kuwa mchafu kwa kumpaka uongo.

kwa moyo wangu wote

Hapa "moyo" unawakilisha nia ya mtu. "kwa umakini kamili" au "kabisa"

Mioyo yao imefanywa kuwa migumu

Hapa "mioyo" inawakilisha nia za watu. Mtu kuwa msumbufu inazungumziwa kana kwamba mioyo yao au nia zao ni ngumu kama jiwe. ""Ni wakaidi"

Psalms 119:71

Maagizo kutoka mdomoni mwako ni

Hapa "mdomo" unawakilisha anachosema Mungu. "Maagizo uliyozungumza ni" au Maagizo yako ni"

ya maelfu ya vipande vya dhahbu na shaba

"ya kiasi kikubwa cha fedha" au "utajiri mkubwa"

Psalms 119:73

YOD

Hili ni jina la herufi ya kumi ya alfabeti ya Kihebrania. Katika lugha ya Kihebrabia, kila mstari wa msistari ya 73-80 unaanza na herufi hii.

Mikono yako imeniumba na kunitengeneza

Mungu kumuumba mtu inazungumziwa kana kwamba Mungu alitumia mikono yake kumuunda mtu kama mtu anavyounda chombo cha udongo.

Mikono yako

Hapa "mikono" inawakilisha nguvu au matendo ya Mungu. "Wewe"

kwa sababu napata matumaini katika neno lako

Hapa "neno" linawakilisha anachosema Mungu. "kwa sababu ninaamini unachosema" au "ninaamini kwa ujasiri unachosema"

Psalms 119:75

katika uaminifu wako umenitesa

"umeniadhibu kwa sababu wewe ni mwaminifu." Mungu anaahidi kuwapa dhawabu wenye haki na kuwaadhibu watenda maovu, kwa hiyo ni mwaminifu kufanya alichosema atafanya.

mtumish wako

Mwandishi anajieleza kama "mtumishi wako." mimi, mtumishi wako" au "mimi"

Psalms 119:77

Acha wenye kiburi waaibishwe

"Waaibishe wenye kiburi" au "sababisha wale wenye kiburi waaibike"

wenye kiburi

"watu wenye kiburi" au "wale wenye kiburi"

Psalms 119:79

geuka kwangu

Watu kumrudia urafiki mwandishi inazungumziwa kana kwamba wanamgeukia yeye kimwili. "njoo kwangu" au "ungana na mimi"

wale wanaojua amri zako za agano

Maana zinazowezekana ni 1) hii inaendelea kuelezea wale wanaomheshimu Mungu au 2) hii inaashiria kusudi la wale wanaomheshimu Mungu kurudi kwa mwandishi. Maneno "ili kwamba" yanaweza kuongezwa kuashiria hili.. "ili kwamba wajifunze unachowaamuru"

Na moyo wangu usiwe na lawama

Hapa "moyo" unawakilisha mawazo ya mtu na nia yake. "Na nisiwe na lawama"

nisiaibishwe

"nisiaibike"

Psalms 119:81

KAFU

Hili ni jina la herufi ya kumi na moja ya alfabeti ya Kihebrania. Katika lugha ya Kihebrabia, kila mstari wa msistari ya 81-88 unaanza na herufi hii.

Ninamatumaini katika neno lako

Hapa "neno" linawakilisha kile anachokisema Mungu. "Ninaamini kwa ujasiri kile unachosema"

Macho yangu yanashauku ya kuona ahadi yako

Hapa "macho" yanawakilisha mtu mzima. "Nasubiri na kusubiri ili ufanye ulichoahidi kufanya"

Psalms 119:83

Nime kuwa kama kiriba katika moshi

Kiriba huaharibika kinaponing'inizwa muda mrefu kwenye sehemu ya moshi. Mwandishi anajifananisha na kiriba kilichoharibiwa na moshi kusisitiza kuwa anajihisi hana faida.

Hadi lini mtumishi wako avumilie hili, utawahukumu lini wale wanaonitesa?

Mwandishi anatumia swali kumwomba Mungu kuwaadhibu wale wanaomtesa. "Tafadhali usinifanye nisubiri zaidi. Waadhibu wale wanaonitesa."

mtumishi wako

Mwandishi analjielezea kama "mtumishi wako." "lazima ni, mtumishi wako" au "lazima ni"

Psalms 119:85

Wenye kiburi wamechimba mashimo kwa ajili yangu

Wenye kiburi wanatafuta kumshika mwandishi au kumsababisha kumfanya atende uovu. Hii inazungumziwa kana kwamba walikuwa ni wawindaji wanaochimba mashimo kumtega mwandishi kama mnyama.

Wenye kiburi

"Watu wenye kiburi" au "Wale walio na kiburi"

Psalms 119:87

Wamekaribia kuniwekea mwisho wangu duniani

Hii ni njia ya ustarabu ya kuzungumzia mtu kutaka kumuua mtu mwingine. "Wamekaribia kumuua"

Kwa upendo wako thabiti

"Kulingana na upendo wako thabiti." "kwa sababu unanipenda kwa uaminifu"

Psalms 119:89

LAMEDI

-Hili ni jina la herufi ya kumi na mbili ya alfabeti ya Kihebrania. Katika lugha ya Kihebrabia, kila mstari wa msistari ya 89-96 unaanza na herufi hii.

maneno yako milele

Hapa "neno" linawakilisha chochote ambacho Mungu amewasilisha kwa watu. "kile ulichosema kitakuwa kweli milele"

neo lako linawekwa thabiti mbinguni

Hapa "neno" linawakilisha chochote ambacho Mungu amewasilisha kwa watu. Hii inazungumzia kuhusu kile ambacho Mungu amesema kana kwamba ni chombo kinachoweza kusimama imara wima. "kile ulichosema kitakuwa cha kweli mbinguni milele"

kwa vizazi vyote

"kwa vizazi vyote vya baadaye." Hii ni lahaja inayomaanisha "milele"

Psalms 119:91

vitu vyote ni watumishi wako

Vitu vyote vilivyoumbwa vinazungumziwa kana kwamba ni watu wanaoweza kumtumikia Mungu. "vitu vyote vinakutumikia" au "vitu vyote vinatii amri zako"

Psalms 119:93

Kamwe sitasahau

"Daima nitakumbuka"

maana kwa hayo umeniweka hai

Inadokezwa kwamba mwandishi anatii maagizo ya Mungu. "kwa kuwa umeniweka kuwa hai kwa sababu ninazitii"

kwa kuwa natafuta maagizo yako

Kujaribu kutii maagizo ya Mungu inazungumziwa kana kwamba maagizo ni kitu ambacho mtu anatakiwa kutafuta.

Psalms 119:95

nitatafuta kuelewa

"nitajaribu sana kuelewa"

kila kitu kina mipaka yake

"vitu vyote vina mwisho"

amri zako ni pana, zaidi ya mipaka

Amri za Mungu daima kuwa kweli na hakika zinazungumziwa kana kwamba amri za mungu ni kitu kilicho kipana sana hadi hakina mwisho. "lakni amri zako hazina mipaka" au "lakini amri zako ni za milele"

Psalms 119:97

MEMU

Hili ni jina la herufi ya kumi na tatu ya alfabeti ya Kihebrania. Katika lugha ya Kihebrabia, kila mstari wa msistari ya 97-104 unaanza na herufi hii.

amri zako daima zako na mimi

Kuwaza daima kuhusu amri za Mungu inazungumziwa kana kwamba amri ni kitu ambacho mwandishi anakua nacho muda wote.

Psalms 119:101

Nimeweka miguu yangu mbali na njia ya uovu

Kuepuka kufanya kilicho kiovu kinazungumziwa kana kwamba ni kuepuka kutembea kwenye njia ambazo ni za uovu. "Nimeepuka kufanya kilicho cha uovu"

Nimeweka miguu

Hapa "miguu" inawakilisha mtu mzima. "nimejiweka"

nifuate neno lako

"nimetii neno lako"

neno lako

Hapa "neno" linawakilisha amri za Mungu.

Sijageuka pembeni kutoka katika amri zako za haki

Kuendelea kutii amri za haki za Mungu inazungumziwa kana kwamba mwandishi hajageuka kimwili kutoka katika amri za haki. "daima huwa natii amri zako za haki"

Psalms 119:103

Ni matamu kiasi gani maneno yako kwangu, ndio, matamu kuliko asali mdomoni mwangu!

Mwandishi kufurahi katika yale ambayo Mungu anasema inazungumziwa kana kwamba maneno ya Mungu ni chakula yaliyokuwa na ladha nzuri kwa mwandishi. "Maneno yako ni mazuri na yanapendeza!"

ninapata utambuzi

"ninajifunza kutambua kilicho sawa"

kwa hiyo ninachukia kila njia ya uongo

Tabia ya uovu inazungumziwa kana kwamba ni njia.

Psalms 119:105

NUN

Hili ni jina la herufi ya kumi na nne ya alfabeti ya Kihebrania. Katika lugha ya Kihebrabia, kila mstari wa msistari ya 105-112 unaanza na herufi hii.

Neno lako ni taa miguuni mwangu na nuru njiani mwangu

Misemo hii miwili ina maana za kufanana. Inazungumza kuhusu Mungu kumwambia mtu jinsi ya kuishi kana kwamba mtu alikuwa akitembea katika njia na neno la Mungu ni nuru inayomsaidia mtu kuona anapoenda. "Maneno yako yananieleza jinsi ya kuishi"

Neno lako

Hapa "neno" linawakilisha yote ambayo Mungu anwasiliana na watu.

Psalms 119:107

kwa ulivyoahaidi katika neno lako

Hapa "neno" linawakilisha kile ambacho Mungu anawasiliana na watu. "kama ulivyoahidi kufanya"

sadaka za kujitolea za mdomo wangu

Mwandishi anazungumzia ombi lake kana kwamba lilikuwa ni sadaka aliyokuwa akiitoa kwa Mungu. "ombi langu kama sadaka kwako"

za mdomo wangu

Hapa "mdomo" unawakilisha mtu mzima.

Psalms 119:109

Maisha yangu daima yako mkononi mwangu

Hii ni lahaja inayomaanisha maisha ya mwandishi yako hatarini wakati wote. "Adui zangu huwa wanajaribu kuniua"

Sisahau sheria yako

"Daima huwa nakumbuka sheria zako"

Waovu wameweka mtego mbele yangu

Watu waovu kujaribu kumshika na kumuua mwandishi inazungumziwa kana kwamba ni wawindaji wanaanda mtego kumshika mnyama.

Waovu

"Watu waovu"

Sijapotea kutoka kwenye maagizo yako

Kutokaidi maagizo ya Mungu inazungumziwa kana kwamba mwandishi hajatembea mbali na maagizo ya Mungu. "Ninatii maagizo yako"

Psalms 119:111

Ninadai amri zako za agano kama urithi wangu milele

Mwandishi kutunza na kutii amri za Mungu inazungumziwa kana kwamba amri ni nchi au mali ambayo mwandishi atarithi. "Sheria zako zitakuwa zangu milele" au "Amri zako za agano ni kama urithi nitakaoutunza milele"

ni furaha ya moyo wangu

Hapa "moyo" unawakilisha mtu mzima. "zinanifanya kuwa na furaha" au "ninazifurahia'

Moyo wangu uko tayari kutii

Hapa "moyo" unawakilisha nia ya mwandishi. Msemo "Moyo wangu uko tayari" ni lahaja. Ni njia ya kusema mwandishi amekusudia. "Nimekusudi kutii"

hadi mwisho

Maana zinazowezekana ni 1) "kila moja" 2) "hadi mwisho wa maisha yangu" au 3) "hadi mwisho wa wakati"

Psalms 119:113

SAMEKHI

Hili ni jina la herufi ya kumi na tano ya alfabeti ya Kihebrania. Katika lugha ya Kihebrabia, kila mstari wa msistari ya 113-120 unaanza na herufi hii.

wenye akili mbili

Mtu asiye mkweli na kuwa na msimamo wa kumtii Mungu anazungumziwa kana kwamba ni mwenye akili mbili. "wasio na msimamo kabisa wa kukutii wewe" au "wasio wakweli"

maficho yangu

Mungu kumfanya mwandishi salama kunazungumziwa kana kwamba Mungu ni sehemu ambayo mwandishi anaweza kwenda na kujificha.

ngao yangu

Mungu kumlinda mwandishi kunazungumziwa kana kwamba Mungu alikuwa ni ngao ya mwandishi.

nasubiri neno lako

Hapa "kusubiri" inamaanisha kusubiri kwa kutarajia. Hii ina wazo la kutumaini au kuamini. "ninatumaini neno lako"

neno lako

Hapa "neno" linawakilisha kile ambacho Mungu anawasiliana kwa watu.

Psalms 119:115

Unitunze kwa neno lako

"Nishikilie kwa neno lako." Hapa "neno" linawakilisha kile ambacho Mungu anawasiliana kwa watu. "Nipe nguvu kama ulivyosema utafanya" au "Niwezeshe kuwa na nguvu kama ulivyoahidi"

na nisiaibike kwa tumaini langu

Hapa "tumaini langu" linawikilisha tumaini la mwandishi kwa Mugnu na ahadi zake. "Usinivunje matumaini." au "Usinisababishe niwe na aibu kwa kutokufanya kile ulichoahidi kufanya."

Psalms 119:117

Unisaidie mimi

"Nisaidie" au "Nitie nguvu"

watu hao ni waongo na sio wa kutegemea

Maana zinazowezekana ni 1) "watu hao wanadanganya na hakuna mtu anayeweza kuwaamini" au 2) "watu hao wanapanga mipango ya uongo lakini watashindwa"

Psalms 119:119

Unawaondoa waovu wote duniani kama takataka

Hapa "takataka" ni yale mabaki yanayobaki wakati wa kusafisha dhahabu au madini mengine ya chuma. Yahwe anawaondoa watu waovu kana kwamba ni takataka.

waovu

"watu waovu"

kama takataka

"kama uchafu"

Mwili unatetemeka kwa kukuogopa wewe

Hapa "mwili" unawakilisha mtu mzima. "Ninatetemeka kwa sababu ninakuogopa"

ninaogopa amri zako za haki

Inadokezwa kwamba mwandishi anaogopa amri za haki za Mungu kwa sababu Mungu anajua kuwa Mungu huwaadhibu wale wanaokaidi amri zake.

Psalms 119:121

AYINI

Hili ni jina la herufi ya kumi na sita ya alfabeti ya Kihebrania. Katika lugha ya Kihebrabia, kila mstari wa msistari ya 121-128 unaanza na herufi hii.

usiniache kwa wakandamizaji wangu

"usiwaruhusu watu wanikandamize"

Hakikisha ustawi wa mtumishi wako

Mwandishi anajizungumzia kama "mtumishi wako." "Hakikisha ustawi wangu" au "Nisaidie na unilinde mimi, mtumishi wako"

wenye kiburi

"wale walio na kiburi" au "watu wenye kiburi"

Psalms 119:123

Macho yangu yanachoka ninaposubiri

Hapa "macho" yanawakilisha mtu mzima. "Ninachoka kwa sababu ninasubiri na kusubiri"

kwa wokovu wako na kwa neno lako la haki

"ili uniokoe kama ulivyoahidi kufanya"

neno lako la haki

Hapa "neno" linawakilisha kile ambacho Mungu anawasiliana na watu. "ahadi yako ya haki"

Mwoneshe mtumishi wako

Mwandishi anajizungumzia mwenyewe kama "mtumishi wako." "Nioneshe" au "Nioneshe mimi, mtumishi wako"

uaminifu wako wa agano

"kwamba unanipenda kwa uaminifu" au "kwa kuwa wewe ni mwaminifu kwangu kwa sababu ya agano lako"

Psalms 119:125

nipe uelewa

"niwezeshe kuelewa kile unachotaka nijue"

Ni muda wa Yahwe kutenda

Mwandishi anazungumza na Yahwe katika hali ya mtu wa tatu. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya mtu wa pili. "Ni muda wako kutenda, Yahwe"

watu wamevunja sheria yako

Hii ni lahaja. Hapa "wamevunja" inamaanisha "kukaidi." Hii ni njia ya kusema kuwa watu wamekaidi sheria ya Mungu.

Psalms 119:127

Ninafuata maagizo yako yote kwa makini

Mtu kutii kwa makini maagizo yote ya Mungu inazungumziwa kana kwamba maagizo yanamwongoza mtu na mtu anayafuata kwa nyuma. "Ninatii kwa makini maagizo yako yote"

kila njia ya uongo

Watu kufanya kilicho kiovu inazungumziwa kana kwamba wanatembea njia mbaya. "njia zote mbaya ambazo baadhi ya watu huishi"

Psalms 119:129

PE

Hili ni jina la herufi ya kumi na saba ya alfabeti ya Kihebrania. Katika lugha ya Kihebrabia, kila mstari wa msistari ya 129-136 unaanza na herufi hii.

Ufunuo wa maneno yako hutoa mwanga

Mwandishi anazungumzia neno la Yahwe kana kwamba maneno hayo nikitambaa kilichokunjwa, na mtu anayefafanua maneno ya Yahwe kana kwamba wanafunua hicho kitambaa. "Ufafanuzi wa maneno yako hutoa mwanga" au "Mtu akifafanua maneno yako, hutoa mwanga"

Ufunuo wa maneno yako hutoa mwanga

Mwandishi anazungumzia maneno ya Yahwe kutoa hekima na mtu kana kwamba maneno yanatoa mwanga kwao. "Ufafanuzi wa maneno yako huwapa watu hekima"

Psalms 119:131

Ninafungua mdomo wangu na kuhema, kwa kuwa nina shauku na amri zako

Mwandishi anazungumzia hamu yake ya amri za Yahwe kana kwamba alikuwa mbwa anayehema kwa ajili ya maji. "nina shauku ya kweli na amri zako"

Nigeukie

Kumgeukia mtu inamaanisha kuvuta nadhari kwa mtu huyo. "Nizingatie"

wanaolipenda jina lako

Hapa neno "jina" linamwakilisha yahwe mwenyewe. "wanaokupenda"

Psalms 119:133

Ongoza hatua zangu

Hapa neno "hatua" inamwakilisha mwandishi anavyotembea. Anazungumzia jinsi anavyoishi, au mwenendo wake, kana kwamba alikuwa akitembea katika njia. "Niongoze" au "Nifundishe jinsi ya kuishi"

usiache dhambi yoyote initawale

Mwandishi anazungumzia dhambi kana kwamba ni mtu mwenye mamlaka juu yake. Maana zinazowezekana ni 1) "usiniache nifanye dhambi yoyote kwa mazoea" au 2) "usiache watu wenye dhambi wanitawale"

Niokoe na ukandamizaji wa wanadamu

"Niokoe na watu wanaowakandamiza wengine"

Psalms 119:135

Acha uso wako ung'ae kwa mtumishi wako

Mwandishi anamzungumzia Yahwe kutenda kwa fadhila kwake kana kwamba uso wa Yahwe ulitoa mwanga juu yake. "Tenda kwa fadhila kwa mtumishi wako"

Mikondo ya machozi

Mwandishi anazungumzia machozi yake mengi kana kwamba ni mkondo wa maji. "Machozi mengi"

hawafuati sheria yako

"hawatii sheria yako"

Psalms 119:137

TSHADE

Hili ni jina la herufi ya kumi na nane ya alfabeti ya Kihebrania. Katika lugha ya Kihebrabia, kila mstari wa msistari ya 137-144 unaanza na herufi hii.

amri za agano

Maana zingine zinazowezekana ni "shuhuda" au "sheria."

Psalms 119:139

Hasira imeniangamiza

Hii ni lahaja. Msemo huu ni kukuza kwa neno na ni njia nyingine ya kusema "Nina hasira sana."

limejaribiwa sana

"Nimelijaribu neno lako mara nyingi"

mtumishi wako hulipenda

Mwandishi anajizungumzia kana kwamba alikuwa ni mtu mwingine. "mimi, mtumishi wako, hupenda" au "ninapenda"

Psalms 119:141

Mimi ... ninachukiwa

"Watu wananichukia"

Psalms 119:143

huzuni na maumivu yamenipata

Mwandishi anazungumzia huzuni na maumivu kana kwamba ni watu. "Nimekuwa na huzuni na maumivu" au "mwili wangu na akili yangu zinateseka"

Psalms 119:145

QOPHU

Hili ni jina la herufi ya kumi na tisa ya alfabeti ya Kihebrania. Katika lugha ya Kihebrabia, kila mstari wa msistari ya 145-152 unaanza na herufi hii.

kwa moyo wangu wote

Mwandishi anajizungumzia mwili ukamili wake kana kwamba ni moyo wake tu. "kabisa"

amri za agano

Maana zingine zinazowezekana ni "shuhuda" au "sheria"

Psalms 119:147

mapambazuko ya asubuhi

"kabla jua halijatokea"

Macho yangu yako wazi kabla usiku haujabadilika

Hii ni lahaja. Katika utamaduni wa Kihebrania, usiku uligawanyika mara tatu. "Niko macho usiku kucha"

Psalms 119:149

Sikia sauti katika uaminifu wako wa agano

Mwandishi anazungumzia anachokisema kana kwamba ni sauti anayotumia kuzungumzia. "Sikia ninachosema kwa sababu ya uaminifu wako wa agano"

wako mbali na sheria yako

"wamepotoka mbali na sheria yako" au "hawazingatii sheria zako"

Psalms 119:151

amri zako zote ni za uaminifu

"ninaweza kuamini amri zako"

amri za agano

Maana zingine zinazowezekana ni "shuhuda" au "sheria"

umeziandaa

Mwandishi wa zaburi anazungumzia amri za Yahwe kana kwamba ni nguzo zilizopangwa kwenye ardhi. "umewapa watu kutii"

Psalms 119:153

RESHI

Hili ni jina la herufi ya ishirini ya alfabeti ya Kihebrania. Katika lugha ya Kihebrabia, kila mstari wa msistari ya 153-160 unaanza na herufi hii.

Angalia mateso yangu

Mwandishi wa zaburi anazungumzia mateso kana kwamba ni kitu ambacho watu wanaweza kuona. "Ona jinsi ninavyoteseka"

Tetea haja yangu

"Nitetee dhidi ya wale wanao nishutumu"

niweke

"linda maisha yangu" au "nipe uhai"

Psalms 119:155

Wokovu u mbali na waovu

mwandishi anazungumzia wokovu kana kwamba ni kitu chenye umbo. "Hakika hautawaokoa waovu"

Matendo yako ya huruma ni mengi

"Umeonesha huruma kwa watu mara nyingi" au "Umefanya matendo mengi ya huruma"

kama hufanyavyo

Maana nyingine inayowezekana ni "kwa sababu unafanya kilicho cha haki"

Psalms 119:157

Watesi wangu

"Wale wanaonitesa mimi"

sijageuka

Hii ni lahaja. "Sijaacha kutii" au "Sijaacha kuamini"

amri za agano

Maana zingine zinazowezekana ni "shuhuda" au "sheria."

waongo

"watu waongo" au "wale wanaonisaliti" au "adui zangu"

hawatunzi

"hawatii"

Psalms 119:159

Tazama

"Angalia" au "Niangalie ili uone"

Asili ya neno lako ni ukweli

"Neno lako ni kweli kabisa" au "Neno lako linaweza kuaminika"

Psalms 119:161

SHINI

Hili ni jina la herufi ya ishirini na moja ya alfabeti ya Kihebrania. Katika lugha ya Kihebrabia, kila mstari wa msistari ya 161-168 unaanza na herufi hii.

moyo wangu unatetemeka, ukiogopa kutokutii neno lako

Mwandishi anazungumzia moyo kana kwamba unaweza kutetemeka na kuogopa. Moyo ni njia nyingine ya kusema mtu mzima. "Ninatetemeka kwa sababu ninaogopa kuwa nitakaidi neno lako"

mapato

Maana zinazowezekana ni 1) vitu ambavyo askari huchukua kwa wale waliowashinda katika vita au 2) vitu vya thamani kubwa au "hazina."

Psalms 119:163

chukia na kinyongo

Maneno haya mawili inamaanisha karibu kitu kimoja. "nachukia sana"

uongo

maana zinazowezekana ni njia nyingine ya kusema 1) "watu wanaodanganya" au 2) "vitu vya uongo ambavyo watu wanasema"

Psalms 119:165

hakuna kitu kinachowafanya wajikwae

Maana zinazowezekana ni 1) "hakuna kitu kinachowafanya kufanya kosa" au 2) "hakuna kitu kinachowaletea shida"

Psalms 119:167

Ninafuata amri zako makini

"Ninatii amri zako makini"

amri zako makini

Maana zingine zinazowezekana ni "shuhuda" au "sheria."

Ninatunza maagizo yako

"Ninatii maagizo yako"

Psalms 119:169

TAVI

Hili ni jina la herufi ya ishirin na mbiliya alfabeti ya Kihebrania. Katika lugha ya Kihebrabia, kila mstari wa msistari ya 169-176 unaanza na herufi hii.

nipe uelewa katika neno lako

Mwandishi anazungumzia uwezo wa kuelewa kana kwamba ni kitu chenye umbo. "nisaidie nielewe neno lako"

Ombi langu lifike mbele yako

Mwandishi wa zaburi anazungumzia maneno anayoyasema kana kwamba ni watu wanaotaka kuzungumza kwa mfalme. "Na usikie ombi langu"

Psalms 119:171

Midomo yangu imwage sifa

Mwandishi wa zaburi anazungumzia midomo yake kana kwamba ni chombo na ni kimiminiko kinachoweza kumwagwa. Hapa neno "midomo" ni neno lingine linalowakilisha mtu mzima. "Ninatamani kukusifu sana"

ulimi wangu uimbe

Mwandishi anazungumzia ulimi wake aidha 1) kana kwamba ni mtu au 2) kama neno lingine la kuwakilisha yeye mzima. "mimi naimba"

Psalms 119:173

Mkono wako unisaidie

Mkono unawakilisha mtu mzima. "Tafadhali nisaidie"

nimechagua

"nimechagua kutii"

ukombozi wako

"unaniokoa"

sheria yako ni furaha yangu

"Ninafurahi sana kutii neno lako"

Psalms 119:175

amri zako za agano zinisaidie

Mwandishi anazungimzia amri za Yahwe kana kwamba ni mtu anayeweza kumsaidia. "naomba nisikilize amri zako za haki ili niwe na hekima na thabiti"

Nimezurura kama kondoo aliyepotea

"nimeacha njia yako kama kondoo aliyeacha kundi lake"

mtafute mtumishi wako

"kwa sababu mimi ni mtumishi wako, njoo unitafute"

Psalms 120

Psalms 120:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

wimbo wa upaaji

Maana zinazowezekana ni 1) "wimbo ambao watu waliimba walipokwenda Yerusalemu kusherehekea" au 2) "wimbo watu walioimba wakati wakipanda ngazi kwenda hekaluni" au 3) "wimbo ambao maneno yake ni kama ngazi."

Katika dhiki yangu

"katika taabu yangu" au "Wakati niko kwenye taabu"

Okoa maisha yangu

Hapa neno "maisha" linamwakilisha mtu. "Niokoe"

kwa wale wanaodanganya na midomo yao na kupotosha na ndimi zao

Hapa msemo "midom yao" na "ndimi zao" inawakilisha watu wanaozungumza uongo na kupotosha. "wale wanao nidanganya na kujaribu kunipotosha"

Psalms 120:3

Atakuadhibuje, na nini zaidi atafanya kwako, wewe mwenye ulimi wa udanganyifu?

Mwandishi anauliza swali hili kama mwongozo wa kueleza kitu ambacho Mungu atafanya kwa waongo. Swali linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Hivi ndivyo Mungu atakavyo kuadhibu, hiki ndicho atakachofanya kwako, wewe mwenye ulimi wa udanganyifu."

wewe mwenye ulimi wa udanganyifu

Hapa "ulimi wa udanganyifu" inamwakilisha mtu anayezungumza uongo. "wewe unayesema uongo"

Atakuadhibu kwa mishale ya shujaa

Mwandishi anazungumzia Mungu kuwaadhibu kwa ukali waongo kana kwamba Mungu anawapiga kwa mishale. "Atakuadhibu kwa ukali, kana kwamba anawapiga kwa mishale ya shujaa"

iliyochongwa juu ya makaa ya moto ya mti wa mfagio

Hii inamaansiha jinsi watu walivyounda ncha ya mshale katika moto. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "aliyochonga juu makaa ya moto ya mti wa mfagio"

Psalms 120:5

Ninaishi Mesheki kwa muda; Niliishi kwa muda katika mahema ya Kedari

sehemu hizi mbili zilikuwa mbali. Mwandishi inawezekana anatumia majina kwa balagha kuashiria kuishi miongoni mwa watu wakatili. "Ni kana kwamba ninaishi Mesheki au katika mahema ya Kedari"

mahema ya Kedari

Msemo huu unawakilisha watu wa Kedari wanaoishi katika mahema hayo. "watu wanaoishi Kedari"

Mimi ni wa amani

"Ninataka amani"

wao ni wa vita

"wanataka vita"

Psalms 121

Psalms 121:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

wimbo wa upaaji

Maana zinazowezekana ni 1) "wimbo ambao watu waliimba walipokwenda Yerusalemu kusherehekea" au 2) "wimbo watu walioimba wakati wakipanda ngazi kwenda hekaluni" au 3) "wimbo ambao maneno yake ni kama ngazi."

nitainua macho yangu

Msemo huu unamaanisha "kutazama" au "kuvuta macho kwa"

Msaada wangu utatoka wapi?

Mwandishi anatumia swali kuvuta nadhari katika chanzo cha msaada wake. Swali hili la balagha linaweza kuelezwa kama kauli. "Nitakwambia msaada wangu unatoka wapi."

Msaada wangu unatoka kwa Yahwe

Hili ni jibu la swali lililopita.

Psalms 121:3

Taarifa ya Jumla:

Hapa ni uhamisho kwenda katika hali ya mtu wa pili. Hii inaweza kumaanisha 1) mwandishi anaanza kuzungumza na wtu wa Israeli au 2) mwandishi anamnukuu mtu mwingine akizungumza na mwandishi.

mguu wako kuteleza

Kuteleza kwa mguu kunahusishwa na kuanguka. "wewe kuanguka"

yeye anayekulinda ... mlinzi

Misemo hii miwli inamaana kitu kimoja, na inasisitiza nafasi ya Mungu kama mlinzi.

yeye anayekulinda hatalala

Hapa "kulala" inamaanisha kuacha kulinda. Hali yake hasi inaimarisha msemo. "Mungu hatalala na kuacha kuwalinda" au " Mungu atawalinda daima"

hatalala ... huwa halali wala kusinzia

Misemo hii miwli inamaana sawa. Msemo wa pili unaimarisha wazo la kwanza.

Tazama

Neno hili linatufanya kuzingatia kwa makini taarifa zinazofuata.

huwa halali wala kusinzia

Mananeo haya mawili yana maana sawa. Hapa "kulala" inamaana kuacha kulinda. Hali yake hasi inaimarisha msemo. "hatalala na kuacha kuwalinda" au "atawalinda daima"

Psalms 121:5

Yahwe ni kivuli katika mkono wako wa kuume

Hapa "kivuli" inamaanisha ulinzi. "Mungu yuko pembeni yako kukulinda dhidi ya vitu vinavyoweza kukudhuru"

mkono wako wa kuume

Hapa msemo huu unamaanisha kuwa pembeni au karibu na mwandishi.

Jua halitakudhuru mchana, wala mwezi usiku

Maneno haya ya tofauti ya "mchana" na "usiku" yanamaanisha tofauti hizo mbili na kila kitu katikati. "Mungu anakulinda na vitu vyote wakati wote"

wala mwezi usiku

Inadokezwa kuwa "hautakudhuru" ndio inadokezwa hapa. Maana kamili ya sentensi hii inaweza kuwekwa wazi. "wala mwezi hautakudhuru usiku"

Psalms 121:7

Yahwe atakulinda ... atalinda maisha yako ... Yahwe atakulinda

Misemo hii ina maana ya kufanana. Kurudia kunaimarisha mawazo.

maisha yako

Hii inamaanisha mwandishi. "wewe"

Psalms 122

Psalms 122:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

wimbo wa upaaji

Maana zinazowezekana ni 1) "wimbo ambao watu waliimba walipokwenda Yerusalemu kusherehekea" au 2) "wimbo watu walioimba wakati wakipanda ngazi kwenda hekaluni" au 3) "wimbo ambao maneno yake ni kama ngazi."

Yerusalemu, miguu yetu inasimama ndani ya malango yako!

Mwandishi anasitisha kuzungumza na wasikilizaji wake kwa muda na kuzungumza moja kwa moja na mji wa Yerusalemu. Yerusalemu inasemeshwa kana kwamba ni mtu anayeweza kusikia na kuandika.

miguu yetu inasimama

Hapa "miguu" inamaanisha mtu mzima. "tunasimama"

ndani ya malango yako

Hapa "malango" inamaanisha mji. "ndani yako, Yerusalemu"

Psalms 122:4

jina la Yahwe

Hapa "jina" linamaanisha Yahwe mwenyewe. "Yahwe"

nyumba ya Daudi

Hapa "nyumba" inamaanisha uzao wa Daudi. "uzao wa Daudi"

Psalms 122:6

Wale wanaokupenda wawe na amani ... amani ndani ya ngome yenu

Sehemu hii inaeleza ujao wa maombi ambayo mwandishi anataka wasikilizaji wake waombe. Anawaomba kuzungumza moja kwa moja na mji wa Yerusalemu, kana kwamba mji ni mtu anayeweza kuwasikia.

Iwepo amani ndani ... iwepo amani ndani

Misemo hii miwili ina maana sawa na pamoja kuimarishana. "watu wa Yerusalemu waishi kwa amani"

ndani ya kuta inayowalinda ... ndani ya ngome yenu

Hapa Yerusalemu inaelezewa kwa kuta zinazoilinda. "ndani ya Yerusalemu"

Psalms 122:8

Taarifa ya Jumla:

Katika sehemu hii, mwandishi anazungumza moja kwa moja na mji wa Yerusalemu, kana kwamba mji ni mtu anayeweza kuwasikia.

Kwa ajili yako

"Kwa faida yako"

Kuwe na amani ndani yako

"Ninaomba kwamba watu ndani yako waishi kwa amani"

nitatafuta mema kwa ajili yako

Nomino dhahania ya "mema" inaweza kuelezwa kama kitendo. "natama kwamba watu wawatende wema"

Psalms 123

Psalms 123:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

wimbo wa upaaji

Maana zinazowezekana ni 1) "wimbo ambao watu waliimba walipokwenda Yerusalemu kusherehekea" au 2) "wimbo watu walioimba wakati wakipanda ngazi kwenda hekaluni" au 3) "wimbo ambao maneno yake ni kama ngazi."

Nainua macho yangu

Hapa mwandishi anamaanisha macho yake kwa sababu ndiyo sehemu ya mwili inayotumika kuonea. "Nitakutazama"

umesimikwa

kuketi kwenye kiti cha enzi na kutawala kama mfalme

kama macho ya mtumishi ... kama macho ya mjakazi ...kwa hiyo macho yetu yanatazama

Misemo hii mitatu inamaana ya kufanana. Msemo wa tatu, unaohusu Waisraeli, unalinganishwa na jinsi watumishi na wajakazi wanavyowatazama bwana zao na bimkubwa wao kwa ajili ya msaada. "Macho" yanaashiria mtu mzima.

mkono wa bwana ... mkono wa bimkubwa

Hapa "mkono" unaashiria utoaji wa mahitaji. "utoaji wa bwana ... utoaji wa bibi"

wajakazi

"watumishi wasichana"

bimkubwa

mwanamke mwenye mamlaka juu ya watumishi wasichana.

awe na huruma kwetu

Nomino dhahania ya "huruma" inaweza kuelezwa kama kitendo. "kutendea kwa huruma"

Psalms 123:3

Uwe na huruma kwetu

Nomino dhahania ya "huruma" inaweza kuelezwa kama kitendo. "kutendea kwa huruma"

tumeshiba ... Tumeshiba zaidi

Misemo hii miwili inamaana ya kufanana, wa pili unaongeza ukali wa ile wa kwanza.

tumeshiba aibu

Hapa aibu inazungumziwa kana kwamba ni kitu kinachoweza kumjaa mtu. "tumefedheheka sana"

Tumeshiba zaidi

Lahaja hii inamaanisha idadi imezidi kwa ubaya. "tumepata kingi sana"

kejeli ... na dharau

Misemo hii miwili inamaana ya kufanana na inatumika pamoja kusisitiza jinsi gani walivyo dhihakiwa na watu.

kejeli

kudhihaki au kutukana

jeuri

Hii inaashiria watu wenye jeuri. "watu wasio na adabu na wenye kiburi"

wenye kiburi

Hii inaashiria watu wenye kiburi. "watu walio na kiburi"

Psalms 124

Psalms 124:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

wimbo wa upaaji

Maana zinazowezekana ni 1) "wimbo ambao watu waliimba walipokwenda Yerusalemu kusherehekea" au 2) "wimbo watu walioimba wakati wakipanda ngazi kwenda hekaluni" au 3) "wimbo ambao maneno yake ni kama ngazi.

Kama Yahwe asingekuwa upande wetu ... basi wangetumeza tukiwa hai

Hii ni kauli ya nadharia tete inayoeleza matokeo ambayo hayakutokea, kwa sababu Yahwe alikuwa upande wao. "Yahwe alikuwa upande wetu ... kwa hiyo hawakuweza kutumeza tukiwa hai"

Kama Yahwe asingekuwa upande wetu ... kama asingekuwa Yahwe aliyekuwa upande wetu

Misemo hii miwili inamaana moja. "Bila msaada wa Yahwe ... bila msaada wa Yahwe"

wangetumeza tukiwa hai

Sitiari hii inaeleza jinsi Waisraeli ambavyo wangeweza kufa kama mnyama mkali anavyoshambuli mnyama mdogo kumla. "wangetuua"

hasira yao ilipowaka dhidi yetu

Hapa "hasira yao" inamaanisha adui waliokuwa na hasira. "walikuwa wametukasirikia sana"

Psalms 124:4

Taarifa ya Jumla:

Katika mistari hii miwili mwandishi anafananisha adui wa Israeli na mafuriko ya maji.

Maji yangetubeba ... yangetuzamisha

Hii inaendela kauli ya nadharia tete kutoka mstari uliopita. Inaeleza matokeo ambayo hayakutokea, kwa sababu Yahwe alikuwa upande wao. "Maji hayakutubeba ... hayakutuzamisha"

Maji ... mbubujiko wa nguvu ... maji ya nguvu

Misemo hii ina maana sawa.

yangetubeba ... ungetulemea ... yangetuzamisha

Misemo hii ina maana sawa.

Maji yangetubeba

Hapa adui wa Mwandishi wanazungumziwa kana kwamba ni mafuriko ya mji. "Adui zetu wangetushinda kwa urahisi"

mbubujiko wa nguvu ungetulemea

Hapa adui wa Mwandishi wanazungumziwa kana kwamba ni mafuriko ya maji ambayo yangewazamisha Waisraeli. "adui zetu wangetulemea"

maji ya nguvu yangetuzamisha

Hapa adui wa Mwandishi wanazungumziwa kana kwamba ni mto wenye hasira kali ambao ungewazamisha Waisraeli. "adui zetu wangetuangamiza"

Psalms 124:6

kuchanwa na meno yao

Adui wanazungumziwa kana kwamba ni wanyama pori ambao wangewaangamiza Waisraeli kwa kuwala. "tuangamizwe kana kwamba tunaliwa na wanyama pori"

tumetoroka kama ndege kutoka kwenye kitanzi cha wawindaji wa ndege

Mwandishi anaelezea kutoroka kwake kutoka kwa adui zake kana kwamba likuwa ndege aliyetoroka kwenye mitego ya wawindaji. "tumetoroka kutoka kwa adui zetu kama ndege anavyotoroka mtego ambao mwindajia ametega"

kitanzi

mtego mdogo wa kamba au uzi unaotengenezwa kukamatia wanyama wadogo au ndege

kitanzi kimekatika

Mpango wa adui kumshika mwandishi umeshindwa kana kwamba ni kitanzi kilicho katika.

Psalms 125

Psalms 125:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kihebrania.

wimbo wa upaaji

Maana zinazowezekana ni 1) "wimbo ambao watu waliimba walipokwenda Yerusalemu kusherehekea" au 2) "wimbo watu walioimba wakati wakipanda ngazi kwenda hekaluni" au 3) "wimbo ambao maneno yake ni kama ngazi."

Wale wanaomtumaini Yahwe ni kama mlima Sayuni, hautikisiki, hudumu milele

Watu wanaomuamini Yahwe wanazungumziwa kana kwamba ni mlima Sayuni. Milima haiwezi kusogea.

Kama milima inavyoizunguka Yerusalemu, hivyo hivyo Yahwe anawazunguka watu wake

Ulinzi wa Yahwe unazungumziwa kana kwamba alikuwa ni milima ilyowazunguka. Yerusalemu ilikuwa imezungukwa na milima kadhaa, iliyoilinda dhidi ya mashambulizi. "Kama milima iliyoizunguka Yerusalemu inavyoilinda, kwa hiyo Yahwe anawalinda watu wake"'

sasa na milele

Hapa msemo huu unamaanisha "daima."

Fimbo ya uovu

Hapa fimbo ya uovu inaashiria utawala wa watu waovu. "watu waovu" au "Viongozi waovu"

Psalms 125:4

Fanya wema, Yahwe

Hili ni ombi. Nomino dhahania "wema" inaweza kuelezwa kama tendo. "Yahwe, tafadhali fanya vitu vizuri" au "Yahwe, nakusihi ufanye vitu vizuri"

walio sawa mioyoni mwao

Hapa "mioyoni" inamaanisha hamu. "hamu ya kufanya kilicho sawa"

geukia

Kukataa kumti Yahwe kunazungumziwa kama kugeuka kutoka njia nzuri. "acha kizuri na kwenda"

njia zao zilizopinda

Hapa njia za uovu zinazungumziwa kana kwamba zilikuwa ni njia ambayo haiko wima. "njia zao za uovu"

atawaongoza

Watu wanaongozwa ili kuadhibiwa. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "kuwaongoza ili kuwaadhibu"

Psalms 126

Psalms 126:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kihebrania.

wimbo wa upaaji

Maana zinazowezekana ni 1) "wimbo ambao watu waliimba walipokwenda Yerusalemu kusherehekea" au 2) "wimbo watu walioimba wakati wakipanda ngazi kwenda hekaluni" au 3) "wimbo ambao maneno yake ni kama ngazi."

aliporejesha utajiri wa Sayuni

"alipoifanya Sayuni kufanikiwa tena"

Psalms 126:2

midomo yetu ilijawa na kicheko

Kucheka kunazungumziwa kana kwamba midomo yao ilikuwa ni chombo, na kicheko chao kilikuwa ndani yake. Inaweza kuwekwa wazi kuwa kicheko hiki kilikuwa na mrejesho wa furaha. "tulicheka kwa furaha"

ndimi zetu na kuimba

Kitenzi "kujawa" kinaweza kuelezwa vizuri. Kuimba kunazungumziwa kana kwamba ndimi zao zilikuwa vyombo, na kuimba kulikuwa ndani yake. "ndimi zetu zilijawa na kuimba" au "tuliimba nyimbo za furaha"

wakasema miongoni mwa mataifa

"watu wamataifa walisema miongoni mwao." Kiwakilishi nomino kinatumika kabla ya kutambulisha kinachozungumzia. Hii sio kawaida.

Yahwe alitutendea mambo makuu; tumefurahi sana!

"Tumefurahi sana, kwa sababu Yahwe ametenda mambo makuu kwa ajili yetu!"

Psalms 126:4

wale wanaopanda kwa machozi ... Anatoka akilia ... akileta miganda yake

Mistari hii miwili inausambamba. Sentensi ya pili inamaana sawa na sentensi ya kwanza, lakini inatoa maelezo zaidi.

wale wanaopanda kwa machozi

"wale wanaopanda wakiwa na machozi"

Psalms 127

Psalms 127:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kihebrania.

wimbo wa upaaji

Maana zinazowezekana ni 1) "wimbo ambao watu waliimba walipokwenda Yerusalemu kusherehekea" au 2) "wimbo watu walioimba wakati wakipanda ngazi kwenda hekaluni" au 3) "wimbo ambao maneno yake ni kama ngazi."

kuamka mapema, kukawia kurudi nyumbani

Mtu anayefanya kazi kwa bidii mara nyingi inambidi kuamka mapema asubuhi na kuchelwa kurudi nyumbani usiku.

kula mkate wa kazi ngumu

Hii ni lahaja. Mkate mara nyingi humaanisha chakula anachohitaji mtu kila siku ili kuishi. "fanya kazi kwa bidii kwa ajili ya mahitaji yako ya kila siku"

Psalms 127:3

urithi

"zawadi" au "mali wa dhamani". Watoto kawaida hupokea urithi kutoka kwa wazazi wao. Urithi huenda kutoka kwa wazazi kwenda kwa watoto. Mstari huu unaonesha watoto kama urithi wa wazazi wao.

Kama mishale kwenye mkono wa shujaa, ndivyo walivyo watoto wa ujanani

Mishale ni ya muhimu sana kwa shujaa kwa sababu inamlinda vitani. Watoto wanazungumziwa kana kwamba ni mishale ya shujaa. "Kuwa na watoto wengi kutakulinda"

aliyejaza podo lake nao

Podo ni chombo kwa ajiil ya mishale. Kuwa na watoto wengi kunazungumziwa kana kwamba watoto walikuwa mishale ndani ya podo. "nyumba iliyojaa watoto" au" wato wengi"

Psalms 128

Psalms 128:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kihebrania.

wimbo wa upaaji

Maana zinazowezekana ni 1) "wimbo ambao watu waliimba walipokwenda Yerusalemu kusherehekea" au 2) "wimbo watu walioimba wakati wakipanda ngazi kwenda hekaluni" au 3) "wimbo ambao maneno yake ni kama ngazi."

Amebarikiwa kila mtu anayemheshimu Yahwe

Msemo huu unatoke katika sauti isiyotenda kuashiria kuwa Yahwe halazimiki kumbariki mtu anayemheshimu. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe atambariki kila mtu anayemheshimu"

Kile ambacho mikono yako huleta

Mtu anaweza kutambulika kwa mikono yake kwa sababu hiyo ndio sehemu ya mwili anayotumia kufanyia kazi. "Unacholeta" au "Unachofanyia kazi"

utabarikiwa na kufanikiwa

Maneno "kubarikiwa" na "kufnikiwa" ina maana ya kukaribiana na inasisitiza fadhili za Mungu. "Yahwe atakubariki na kukufanikisha" au "Yahwe atakufanya ubarikiwe na ufanikiwe"

Psalms 128:3

kama mzabibu uzaao ndani ya nyumba yako

Mke anazungumziwa kama mzabibu uzaao matunda mengi. Hii inaashiria kuwa watoto ni kama matunda na mke atakuwa na watoto wengi. "anazalisha sana na atakupa watoto wengi"

watoto wako watakuwa kama mimea ya mizeituni

Watoto wanalinganishwa na mimea ya mizeituni kwa sababu ya jinsi inavyokuwa na kuzunguka kitu. Watoto wataizunguka meza na kuijaza. "utakuwa na watoto wengi watakao kuwa na kufanikiwa"

wakiizungunka meza yako

Hii inamaanisha sehemu ambapo familia hukusanyika kula. Maranyingi, wote wanaokula kwenye meza ya mtu wako chini ya utawala wake.

mtu atabarikiwa anayemheshimu Yahwe

Hii inaweza kuelezwa katika kitenzi cha kutenda. "Yahwe atambariki mtu anayemheshimu"

siku zote za maisha yako

"maishani mwako mwote"

Amani iwe juu ya Israeli

"Israeli iwe na amani"

Psalms 129

Psalms 129:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

wimbo wa upaaji

Maana zinazowezekana ni 1) "wimbo ambao watu waliimba walipokwenda Yerusalemu kusherehekea" au 2) "wimbo watu walioimba wakati wakipanda ngazi kwenda hekaluni" au 3) "wimbo ambao maneno yake ni kama ngazi."

Wakulima wamelima mgongoni mwangu

Mikwaruzo kutokana na kupigwa inazungumziwa kama kulima kwa mkulima. Mkulima alilima mistari yenye kina kirefu kiwanjani. "Adaui zangu wamenikata sana mgongoni mwanga"

wakaifanya mifuo yao kuwa mirefu

Huu ni mwendelezo wa msemo wa ukulima. "Mfuo" ni mstari ambao mkulima aliulima. "walifanya mikwaruzo yao kuwa mirefu"

Psalms 129:4

amekata kamba za waovu

Israeli inazungumziwa kama imefungwa na watu waovu. "ametuokoa na adui zetu"

Wote waaibishwe na kugeuzwa

Yahwe hajatajwa wazi kama ndiye aliyefanya hivi vitu. Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "Yahwe awaaibishe na kuwashinda"

Psalms 129:6

Na wawe kama ... miganda

Mwandishi wa zaburi anawazungumzia adui zake kufa na kuwa wachache kwa idadi. Wanalinganishwa na nyasi ndogo zinazoota kwenye paa ya nyumba na kukauka na haitoshi kukata au kukusanya. "Na wafe na wawe wachache sana hadi wawe kama nyasi ... miganda"

baraka ya Yahwe iwe juu yako

"Yahwe akubariki"

Psalms 130

Psalms 130:1

Taarifa ya Ujumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kihebrania.

wimbo wa upaaji

Maana zinazowezekana ni 1) "wimbo ambao watu waliimba walipokwenda Yerusalemu kusherehekea" au 2) "wimbo watu walioimba wakati wakipanda ngazi kwenda hekaluni" au 3) "wimbo ambao maneno yake ni kama ngazi."

Toka vilindini

Huzuni ya mwandishi inazungumziwa kana kwamba ni chombo. Huzuni yake inatokea chini ya chombo. Huzuni mwara nyingi huzungumziwa kama chombo kinachojaa kutoka juu hadi chini. "Kwa sababu nina huzuni sana,"

acha maskio yako yawe masikivu

Masikio yanaashiria ni Yahwe, lakini kwa sababu mwandishi anafahamu kuwa Yahwe anasikia kila kitu, anachoomba ni kwa Yahwe kujibu. "tafadhali sikiliza" au "tafashali jibu"

kwa maombi yangu ya huruma

"Huruma" sio kitu kinachoweza kupewa kimwili kwa mtu. Mwandishi anazungumzia kuhusu Yahwe kuwa na huruma kwake. "kwa maombi yangu na kuwa na huruma kwangu"

Psalms 130:3

nani atasimama?

Mwandishi anatumia swali hili kuonesha ubatili wa kuwaza kuwa mtu yeyote anaweza kusimama katika hali hii. Hili swali balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "hakuna anayeweza kusimama."

nani atasimama

"Kusimama" mara humaanisha kutoroka au kupona wakati mtu anaposhambulia. Kwa hali hiyo, itamaanisha kutoroka kutoadhibiwa. "hakuna anayeweza kutoroka adhabu yako" au "hakuna anayeweza kupona adhabu yako"

Psalms 130:5

Nafsi yangu

"Nafsi yangu" inamaanisha mwandishi wa zaburi. "mimi"

Nafsi yangu inasubiri

Mwandishi wa zaburi anazungumziwa kana kwamba anasubiri kitu kwa kutarajia. "Natumaini" au "Nina amini" au "Ninatamani kitu"

Nafsi yangu inasubiri ... zaidi ya walinzi wanavyosubiri asubuhi

Mwandishi wa zaburi anazungumzia hamu yake Bwana kumsaidia kama kuwa zaidi ya ile hamu ya wale wanaofanya kazi usiku kucha wakisubiri asubuhi ifike.

walinzi

Hawa ni wanaume wanaolinda miji au viwanja dhidi ya adui na wezi. Hapa inamaanisha watu wanaokeshi uskiu kufanya hivi.

Psalms 130:7

Israeli ... dhambi zake

Watu wa Israeli wanazungumziwa kana kwamba walikuwa ni mtu. "watu wa Israeli ... zao"

Psalms 131

Psalms 131:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

wimbo wa upaaji

Maana zinazowezekana ni 1) "wimbo ambao watu waliimba walipokwenda Yerusalemu kusherehekea" au 2) "wimbo watu walioimba wakati wakipanda ngazi kwenda hekaluni" au 3) "wimbo ambao maneno yake ni kama ngazi."

moyo wangu hauna kiburi au macho yangu majivuno

Moyo na macho yanamwakilisha mtu. "Sina kiburi wala majivuno"

Sina matumaini makubwa kwa ajili yangu

Maana zinazowezekana ni "Sitegemei kufanya mambo makuu" au "Sidhani kuwa mimi ni mkuu"

vitu ambavyo viko njee ya uwezo wangu

Vitu vilivyo vigumu sana kwa mtu kuelewa vinazungumziwa kana kwamba viko nje ya uwezo wa mtu au mbali sana kutoka kwa huyo mtu kuweza kufikia. "vitu vilivyo vigumu sana kuelewa"

Psalms 131:2

Nimetuliza na kunyamazisha nafsi yangu

Nafsi inawakilisha mtu au hisia zake. Kuwa mtulivu na wa amani inazungumziwa kama kufanya nfasi ya mtu kutulia na kuwa kimya. "Nimetulia na nina amani"

nafsi yangu ndani yangu

Nafsi inawakilisha mtu au hisia zake. "mimi"

mtoto aliyeachishwa kifuani mwa mama yake

Mwandishi anajizungumzia kuridhika na kupumzika kana kwamba alikuwa mtoto mchanga ambaye haitaji tena maziwa kutoka kwa mama yake. "kuridhika kama mtoto mchanga ambaye halilii tena maziwa ya mama yake lakini anapumzika mikononi mwake" au "kuridhika na kupumzika"

Psalms 132

Psalms 132:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

wimbo wa upaaji

Maana zinazowezekana ni 1) "wimbo ambao watu waliimba walipokwenda Yerusalemu kusherehekea" au 2) "wimbo watu walioimba wakati wakipanda ngazi kwenda hekaluni" au 3) "wimbo ambao maneno yake ni kama ngazi."

kwa ajili ya Daudi

"kwa sababu ya kilichotokea kwa Daudi"

ita katika kumbukumbu

"kumbuka" au "fikiri kuhusu"

Hodari wa Yakobo

Hii inamaanisha Mungu.

Psalms 132:3

Akasema

"Mfalme Daudi alisema"

Sitayapa usingizi macho yangi wa kupumzika kwa vigubiko vya macho yangu

Usingizi na kupumzika zinazungumziwa kana kwamba ni vitu vinavyoweza kupewa. Hapa macho na vigubiko vya macho vinawakilisha mtu mzima. "Sitaruhusu macho yangu kulala wala vigubiko vya macho yangu kupumzika" au "sitalala wala kufunga macho yangu kupumzika"

hadi nipate sehemu kwa ajili ya Yahwe

Kujenga sehemu kwa ajili ya Yahwe inazungumziwa kama kumtafutia sehemu. "hadi nijenge sehemu kwa ajili ya Yahwe"

Hodari wa Yakobo

Hii inamaanisha Mungu.

Psalms 132:6

tulisikia kuihusu Efrata

Kitu kinachozungumziwa inawezekana ni sehemu ambapo sanduku takatifu la Mungu lilipokuwa. Msemo "Efrata" inawezekana kumaanisha sehemu waliyokuwa wakati wakisikia habari yake. Hii inaweza kuwekwa wazi. "sisi tuliokuwa Efrata tulisikia kuhusu ambapo sanduku takatifu lilipo" au " sisi tulioko Efrata tulisikia kuwa sanduku takatifu lilikuwa Yearimu"

viwanja vya Yearimu

Hii inaweza kumaanisha viwanja vinavyouzunguka mji.

tutaabudu miguuni pake

Kumwabudu Mungu katika sanduku la agano inazungumziwa kama kusujudu kwenye miguu ya mfalme anayeketi katika kiti chake cha enzi. Hii inaonesha unyenyekevu na usikivu kwa Mungu. "tutaenda kwenye sanduku la agano la Mungu na kumwabudu kama mfalme"

Inuka, Yahwe, kwenye sehemu yako ya kupumzikia

Kitenzi "njoo" kinaweza kuelezwa wazi. "Inuka, Yahwe, na uje kewnye sehemu yako ya kupumzika"

sehemu yako ya kupumzikia

Sehemu ambayo Mungu alichagua ya watu kumwabudu inazungumziwa kama sehemu anayopumzikia au anapoishi milele. "sehemu unayokaa" au "hema lako"

wewe na sanduku la nguvu yako!

Maana zinazowezekana ni 1) "njoo kwenye sanduku la nguvu yako" au 2) "njoo, na ufanye sanduku la nguvu yako lije."

sanduku la nguvu yako

"sanduku linaloonesha uwezo wako mkuu"

Psalms 132:9

Makuhani wako wavikwe na uadilifu

Uadilifu unazungumziwa kana kwamba ni nguo. "Watu watambue kuwa makuhani wako wana uadilifu" au "Nataka watu waone kuwa makuhani wako daima hufanya kilicho sawa"

Kwa ajili ya mtumishi wako Daudi

"Kwa sabau ya kilichotokea kwa mtumishi wako Daudi."

usigeuke kutoka kwa mfalme wake aliyetiwa mafuta

Hapa "kugeuka" inamaanisha kumkataa mtu. "usimuache mfalme uliyemtia mafuta"

Psalms 132:11

Nitamweka mmoja wa uzao wako kenye kiti chako cha enzi

Kumfanya uzao wa mfalme kuwa mfalme badala yake inazungumziwa kama kumweka katika kiti cha enzi cha huyo mfalme. "Nitasababisha mmoja wa uzao wako kutawala Israeli katika nafasi yako"

wataketi kwenye kiti chako cha enzi

Kutawala kama mfalme inazungumziwa kama kuketi kwenye kiti cha enzi.

watoto wako

Hapa "watoto wako" inawakilisha uzao wa Daudi watakao kuwa wafalme. "uzao wako"

Psalms 132:13

Taarifa ya Jumla:

Katika mstari wa 13 anayetamani ni Yahwe na mstari wa 14 anayezungumza ni Yahwe. Yule anayetamaniw ni Sayuni.

Sayuni ... amemtamani ... ninmtamani

Mwandishi anaandika kana kwamba mji wa Sayuni ulikuwa ni mwanamke.

amemtamani kwa ajili ya kiti chake

Hapa "kiti" kinaashiri kati ya 1) kiti chake cha enzi atakapotawala, au 2) sehemu atakayo ishi.

amemtamani kwa ajili ya kiti chake

Yahwe ametamani Sayuni kwa ajili ya kiti cha Yahwe." Hii inaonesha washiriki halisi.

sehemu yangu ya kupumzika

Sehemu ambayo Mungu alichagua ya watu kumwabudu inazungumziwa kama sehemu anayopumzikia au anapoishi milele. "sehemu ninayokaa" au "hema langu"

Psalms 132:15

Kauli Unganishi:

Mungu anaendelea kuzungumzia mji wa Sayuni kana kwamba Sayuni ni mwanamke.

Nitambariki sana

"Nitambariki sana Sayuni"

Nitawaridhisha maskini wake kwa mkate

Hapa "maskini" inamaanisha watu maskini waliomo Sayuni. Hapa "mkate" inaweza kumaanisha chakula kwa ujumla. "Nitawaridhisha watu wa Sayuni kwa chakula"

Nitawavika makuhani wake na wokovu

Wokovu unazungumziwa kana kwamba ni nguo. Maana zinazowezekana ni 1) "Nitawasababisha makuhani kuenenda kwa namna inayostahili ya wale niliowaokoa" au 2) "Nitawaokoa makuhani wake"

Psalms 132:17

Nitafanya pembe lichomoze kwa ajili ya Daudi

Mungu anazungumzia mwana mwenye nguvu wa Daudi kana kwamba alikuwa ni pembe lenye nguvu la mnyama. "Nitamfanya mwana wa Daudi awe mfalme baada yake" au "Nitamfanya Daudi awe na mwana katika uzao wake atakaye kuwa mfalme mwenye nguvu"

nitaweka taa kwa ajili ya mtiwa mafuta wangu

Mungu anazungumzia kusabisha uzao wa Daudi kuendelea kutawala kama wafalme kana kwamba walikuwa ni taa inayoendela kung'aa. "Nitafanya uzao wa mtiwa mafuta wangu kuendelea kutawala kama wafalme"

mtiwa mafuta wangu

"mfalme wangu niliye mchagua" au "mfalme niliye mchagua"

Nitawavika adui zake na aibu

Aibu inazungumziwa kana kwamba ni nguo. Aibu hii inatokana na kushindwa vitani. "Nitawafanya adui zake washindwe vitani na waaibike"

taji lake linatang'aa

Taji linawakilisha utawala wake, na ukuu unnazungumziwa kama kung'aa"

Psalms 133

Psalms 133:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

wimbo wa upaaji

Maana zinazowezekana ni 1) "wimbo ambao watu waliimba walipokwenda Yerusalemu kusherehekea" au 2) "wimbo watu walioimba wakati wakipanda ngazi kwenda hekaluni" au 3) "wimbo ambao maneno yake ni kama ngazi."

Tazama

Hili neno linatumika kusisitiza umuhimu wa kauli inayofuata.

kwa ndugu kuishi pamoja

Uhusiano miongoni mwa watu wa Mungu unazungumziwa kama ndugu. "kwa watu wa Mungu kuishi pamoja kwa amani kama ndugu"

Psalms 133:2

Ni kama mafuta mazuri kichwani

Uzuri wa umoja miongoni mwa watu wa Mungu unazungumziwa kana kwamba yalikuwa mafuta mazuri yaliyomwagwa kichwani pa Haruni. "Huu umoja ni wa dhamani kama mafuta yaliyomwagwa kwenye kichwa cha Haruni.

kama umande wa Hermoni

Uzuri wa umoja miongoni mwa watu wa Mungu unazungumziwa kana kwamba ulikuwa umande unaoburudisha. "unaburudisha kama umande wa hermoni"

Hermoni

Huu ni mlima katika Israeli wenye theluji mwaka mzima.

Psalms 134

Psalms 134:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

wimbo wa upaaji

Maana zinazowezekana ni 1) "wimbo ambao watu waliimba walipokwenda Yerusalemu kusherehekea" au 2) "wimbo watu walioimba wakati wakipanda ngazi kwenda hekaluni" au 3) "wimbo ambao maneno yake ni kama ngazi."

watumishi wote wa Yahwe

"wote mnaomtumikia Yahwe"

Inueni mikono yenu

Hivi ndivyo watu walivyoomba au kumsifu Mungu.

kwenye sehemu takatifu

Maana zinazowezekana ni 1) "kwenye hekalu" au 2) "kwenye sehemu takatifu hekaluni"

Psalms 134:3

mbingu na nchi

Msemo "mbigu na nchi" hapa unaashiria vitu vyote. "vitu vyote mbinguni na duniani"

Psalms 135

Psalms 135:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Lisifuni jina la Yahwe

Jina la Yahwe linamwakilisha yeye. "Msifuni Yahwe" au "Msifuni yeye"

simama katika nyumba ya Yahwe

Hii inawakilisha kumtumikia Yahwe hekaluni mwake.

Yahwe ... Mungu wetu

"Mungu wetu" inamaanisha Yahwe.

Psalms 135:3

kwa kuwa ni vyema kufanya hivyo

"kwa sababu tunapata raha kwa kulisifu jina lake"

Yahwe amemchagua Yakobo

"Yakobo" hapa inamaanisha uzao wake, watu wa Israeli. "Yahwe amewachagua uzao wa Yakobo"

Israeli kama mali yake

"ameichagua Israeli kuwa mali yake"

Psalms 135:5

kuwa Bwana wetu yuko juu ya miungu yote

"ninajua kuwa Bwana wetu yuko juu ya miungu yote." Kuwa mkuu zaidi ya kitu inazungumziwa kama kuwa juu yake. "kuwa Bwana wetu ni mkuu zaidi ya miungu yote"

Psalms 135:7

kuleta upepo kutoka kwenye ghala lake

Ghala ni sehemu ambapo vitu hutunzwa kwa ajili ya matumizi ya baadaye. Picha hii inaonesha nguvu ya Mungu kuumiliki upepo. "kuusababisha upepo kupuliza kwa uwezo wake"

Psalms 135:8

ishara na maajabu

Maneno haya mawili yana maana moja na yanamaanisha matatizo ya kimiujiza ambayo Mungu alisababishia Misri.

katikati yenu, Misri

Mwandishi anazungumza kana kwamba watu wa Misri walikuwa wakimsikiliza. "katikati yenu watu wa Misri" au "katikati ya watu wa Misri"

dhidi ya Farao

"kumwadhibu Farao"

Psalms 135:10

Sihoni ... Ogu

Haya ni majina ya wanaume wawili.

Psalms 135:12

Alitupa nchi yao kama urithi

Zawadi ya Mungu ya nchi kwa Wasiraeli inazungumziwa kana kwamba ni urithi kutoka kwa baba kwenda kwa mwana. "Alitupa nchi yao kuwa nayo milele" au "Alitupa nchi yao kuwa yetu milele"

Jina lako

Jina lake hapa linawakilisha umaarufu wake au sifa yake. "Umaarufu wako" au "Sifa yako"

Psalms 135:19

yeye anayeishi Yerusalemu

Mungu anazungumziwa kana kwamba aliishi Yerusalemu kwa sababu hekalu ambalo Waisraeli walimwabudia lilikuwa huko. "yeye ambaye hekalu lake liko Yerusalemu"

Psalms 136

Psalms 136:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

O

Huu ni mshangao.

Mungu wa miungu

Mungu aliye mkuu zaidi ya miungu mingine ambayo watu huabudu.

Psalms 136:4

kwa hekima

Kwa sababu ana hekima.

Psalms 136:6

aliyesambaza dunia juu ya maji

Waisraeli wa zamani walidhani kwamba nchi kavu ya dunia ilikuwa juu ya bahari. "aliyeweka dunia juu ya maji"

taa kuu

Hii inamaanisha vyanzo vya nuru kwa ajili ya dunia, hasa jua na mwezi. "jua na mwezi na nyota"

Psalms 136:8

kutawala machan ... kutawala usiku

Jua, mwezi, na nyota zinazungumziwa kana kwamba ni wafalme. "kuweka alama ya muda wa siku ... kuweka alama ya muda wa usiku"

Psalms 136:10

kutoka miongoni mwao

"kutoka miongoni mwa watu wa Misri"

kwa mkono wenye nguvu na ulioinuka

Hapa "mkono" inawakilisha uwezo. "kwa uwezo mkuu"

Psalms 136:13

bahari la Matete

wanajeshi wa Farao walizama katika bahari la Matete.

akampindua Farao

Hapa kushindwa kunazungumziwa kama kumpindua mtu. "akamshinda Farao" au "akamshinda mfalme wa Misri"

Farao

Jeshi la Farao.

Psalms 136:18

Sihoni ... Ogu

Wafalme hawa walikuwa wafalme wawili tu kati ya wengi ambao Mungu aliwawezesha Waisraeli kuwashinda.

Psalms 136:21

alituita akilini

"alituwaza"

kutusaidia katika aibu yetu

Hali ya kuhisi aibu inazungumziwa kana kwamba ni sehemu ambayo Waisraeli walikuwepo. Hii kumbukumbu ya nyakati nyingi ambapo adui wa israeli walishindwa katika vita na kuwaaibisha. "kutujali wakati tulipoaibishwa"

Psalms 136:24

ametupa ushindi juu adui zetu

Kusababisha watu kuwa washindi na kuwashinda adui zao inazungumziwa kama kuwapa ushindi, kana kwamba ushindi ni kitu kinachoweza kupewa. "ametufnay kuwa washindi juu ya adui zetu" au "ametufanya kuweza kuwashinda adui zetu"

Mungu wa mbinguni

Mungu anayeishi mbinguni" au "Mungu ambaye viumbe wa mbinguni wanamwabudu"

Psalms 137

Psalms 137:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kando ya mito ya Babeli

"Katika mto mmoja karibu na Babeli"

tulikaa ... kulia ... tulipo fikiria ... tulininginiza

Mwandishi hawajumuishi wasomaji.

Katika mpopla huko

Miti ya mpopla haioti Israeli. "Mpopla" hapa inaweza kuwakilisha miti yote Babeli. "Katika miti ndani ya Babeli"

Psalms 137:3

waliotuchukua mateka walitaka nyimbo kutoka kwetu

Hapa "nyimbo" inaashiria vitendo vya kuimba. "waliotuchukua mateka walitaka tuimbe"

walitaka tuwe na furaha

"walitufanya tujifanye kana kwamba tuna furaha"

moja ya nyimbo za Sayuni

Hii inaweza kumaanisha nyimbo ambazo Waisraeli walitumia katika kuabudu hekaluni Yerusalemu.

Psalms 137:5

Nikisahau kumbukumbu yako, Yerusalemu

Mwandishi anazungumza kana kwamba Yerusalemu inamsikiliza. "Nikifanya kana kwamba nimekusahau, Yerusalemu" au "Nikijaribu kukusahau, Yerusalemu"

mkono wa kuume

mkono ambao watu wengi hutumia zaidi

Psalms 137:7

Kuita akilini

"Kukumbuka" au "Kufikiria"

Kuita akilini, Yahwe, walichofanya Waedomu

Hapa kukumbuka kile ambacho Waedomu walichofanya inawakilisha kuwaadhibu kwa kile walichotenda. "Waadhibu Waedomu, Yahwe, kwa kile walichotenda"

siku ambayo Yerusalemu ilianguka

Yerusalemu kukamatwa na jeshi la adui inazungumziwa kana kwamba imeanguka. Aliyeikamata Israeli inaweza kuwekwa wazi. "siku ambayo Yerusalemu ilikamatwa" au "siku ambayo jeshi la Babeli liliingia Yerusalemu"

Psalms 137:8

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anawahutubia watu wa Babeli kana kwamba wanamsikiliza.

Binti wa Babeli

Hii inamaanisha mji wa Babeli na watu wake.

na mtu abarikiwe

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Mungu ambariki mtu"

anayekulipa kwa kile ulichokifanya kwetu

Mwandishi anazungumzia mtu kuwatendea wengine alichotendewa kana kwamba ni malipo. "kufanya kwako ulichofanya kwetu"

kuwaseta wadogo wenu kwenye mwamba

"kuponda vichwa vya watoto wenu kwenye miamba"

Psalms 138

Psalms 138:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Nitakupa shukrani na moyo wangu wote

Hapa moyo unawakilisha hisia. Kufanya kitu kwa dhati au kamili inazungumziwa kama kukifanya kwa moyo wote. "Nitakushukuru kwa dhati"

mbele ya miungu

Maana zinazowezekana ni 1) "licha ya sanamu za uongo zilizopo" au 2) "mbele ya mkusanyiko wa mbinguni," ambayo inamaanisha "katika ufahamu wa malaika mbinguni"

Nitasujudu

Kusujudu ni kitendo cha ishara kinachowakilisha kuabudu au kutoa heshima. "Nitakuabudu"

kutoa shukrani kwa jina lako

"kukupa wewe shukrani"

neno lako

Hii inamaanisha kile ambacho Mungu amesema. "kile ulichosema" au "amri zako na ahadi zako"

jina lako

Maana zinazowezekana ni 1) "mwenyewe" au 2) "umaarufu wako"

Psalms 138:3

Wafalme wote wa ulimwenguni

"Viongozi wote wa duniani"

mdomo wako

Msemo huu unamwakilisha Mungu mwenyewe. "wewe"

Psalms 138:5

Yahwe yuko juu, lakini anawajali walio chini

Yahwe yuko juu ya uumbaji wote katika nguvu, nafasi, na mamlaka. Lakini shauku lake ni kwa wale walio wanyenyekevu wa moyo, watumishi kwa wote. Hii ni tofauti rahisi.

wenye majivuno anawajua kwa mbali

Msemo huu unaweza kuwa unamaanisha kuwa Mungu sio mwaminifu kwa wale wenye majivuno.

Psalms 138:7

natembea

kuishi

katikati ya hatari

Kuwa hatarini inazungumziwa kama kuwa katika sehemu ya kimwili.

utafika na mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu

Mungu anazungumziwa kana kwamba atawapiga adui kwa mkono wake.

hasira ya adui zangu

Hasira inazungumziwa kana kwamba ni kitu badala ya hisia. "adui zangu, ambao wana hasira"

mikono yako imeumba

Mungu anazungumziwa kana kwamba alitumia mikono yake kihalisia kuumba. "umeumba"

wale ambao mikono yako imeumba

Msemo huu unawezekana kumaanisha taifa la Israeli.

Psalms 139

Psalms 139:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

umenichunguza

"umenipima"

ninapoketi na ninapoinuka

Mwandishi wa zaburi anatumia vitendo hivi viwili kuwakilisha kila kitu afanyacho. "kila kitu ninachofanya" au "kila kitu kunihusu mimi"

Psalms 139:3

njia yangu na kulala kwangu

Hapa "njia" inamaanisha tabia. "Njia yangu na kulala kwangu" kwa pamoja zinamaanisha kila kitu kuhusu mwandishi wa zaburi.

kabla kuna neno kwenye ulimi wangu

Hapa "neno kwenye ulimi" linawakilisha maneno. "kabla sijasema kitu"

Nyuma yangu na mbele yangu unanizunguka

Maelezo haya yanamaanisha uwepo wa Mungu kila sehemu.

kuweka mkono wako juu yangu

Msemo huu unamaanisha uongozo na msaada. "unaniongoza na kunisaidia"

mwingi sana kwangu

"mwingi sana kwangu kuelewa"

uko juu sana; na siwezi kuufikia

Kuwa juu na nje ya uwezo ni usemi, kwa hali hii, kuhusu maarifa ambayo wanadamu hawawezi kuwa nao. "ni magumu sana kuelewa"

Psalms 139:7

Naweza kwenda wapi mbali na Roho yako? ... Naweza kuukimbia wapi uwepo wako?

Maswali haya mawili yana usambamba. Mwandishi wa zaburi anasema kwamba hawezi kuepuka uwepo wa Mungu. "Siwezi kuitoroka Roho yako."

nikitengeneza kitanda changu kuzimu

"Kutengeneza kitanda cha mtu" inamaanisha kuishi sehemu. "hata kama nikiishi kuzimu"

Psalms 139:9

Kama nikipaa kwenye mbawa za asubuhi na kwenda kuishi kwenye sehemu za mbali za bahari

Mwandishi aneleza kwamba popote alipo, Mungu yupo pia.

Kama nikipaa kwenye mbawa za asubuhi

Katika sehemu ya zamani karibu na mashariki, jua lilifikiriwa kana kwamba lina mbawa zilizoliwezesha kupaa juu ya anga. "Kama jua lingeweza kunibeba lenyewe juu ya anga"

kwenye sehemu za mbali za bahari

"mbali sana magharibi"

utanishikilia

"utanisaidia"

Psalms 139:11

Kama ningesema, "Hakika giza litanifunika

Mwandishi wa zaburi anazungumzia usiku kana kwamba ni blangeti inayoweza kumfunika.

Usiku utang'aa kama mchana

Usiku, ambao ni giza, unazungumziwa kana kwamba unang'aa mwanga.

Psalms 139:13

Umeunda sehemu zangu za ndani

"Sehemu za ndani" inamaanisha sehemu za ndani za mwili za mtu, lakini usemi huu hapa unaweza kuwa unamaanisha mwili mzima. "Umeumba mwili wangu wote"

Nafsi yangu inatambua hili vizuri

Hapa "nafsi" inaweza kumaanisha uwezo wa ndani wa mwandishi wa zaburi kuwa na uhakika na upendo na uongozo wa Mungu. "Ninajua hili kwa moyo wangu wote'

Psalms 139:15

nilipoumbwa kwa ustadi

"uliniumba kwa ustadi mkubwa"

katika sehemu za chini za nchi

Hii inawezekana kuwa namna kuzungumzia tumbo la mama mzazi.

siku zangu zote nilizopewa ziliandikwa kwenye kitabu chako hata kabla ya kwanza haijatokea

Msemo huu unashiria kuwa Waisraeli wa zamani walifikiri kuwa Mungu aliandika mipango yake kwenye kitabu.

Psalms 139:17

thamani

"muhimu"

Idadi yake ni kubwa kiasi gani!

"Mawazo yako ni mengi sana."

yatakuwa zaidi ya namba ya mchanga

"hayahesabiki"

Psalms 139:19

nendeni mabli na mimi, nyie watu wenye vurugu

Mwandishi wa zaburi anajifanya kuzungumza moja kwa moja na watu wenye vurugu ambao anao akilini.

Wanaasi dhidi wako

"Wanaasi dhidi ya mamlaka yako, Mungu"

adui zako wanasema uongo

"adui zako wanadanganya kukuhusu"

Psalms 139:21

Je, siwachukii wale, Yahwe, wanaokuchukia? Je, siwachukii wale wanaoinuka dhidi yako?

Sentensi hizi mbili zinamaana ya kufanana. Sentensi ya pili inaimarisha wazo la ya kwanza. Maswali yote haya mawili yanaweza kuunda kauli.

wanaoinuka dhidi

kuasi dhidi ya

Psalms 139:23

Nichunguze

Hili ni ombi kwa Mungu kumwambia mwandishi wa zaburi kuhusu mawazo yoyote ya dhambi anayoweza kuwa nayo. "Tafadhali nichunguze" au "Nakuomba unichunguze"

Nichunguze, Mungu, na ujue moyo wangu; nijaribu na ujue mawazo yangu

Sentensi hizi mbili zinamaana ya kufanana. Sentensi ya pili inaimarisha wazo la ya kwanza.

njia yoyote ya uovu

Hapa "njia" inamaanisha tabia.

njia ya milele

Hapa "njia" inamaanisha kumtumaini na kumtii Mungu. Yeyote "anayetembea" hivi atakuwa na maisha ya milele.

Psalms 140

Psalms 140:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

wanasababisha vita

Hapa "vita" inaweza kumaanisha ugomvi wa aina yoyote, yakiwemo mabishano.

Ndimi zao zinaumiza kama nyoka

Watu wanaosababisha ugomvi kwa yale wanayosema wanazungumziwa kana kwamba wana ndimi za nyoka. Ingawa nyoka hawadhuru kwa ndimi zao, lakini kwa kung'ata kwao na hasa kwa sumu. Wala mtu hawezi kuuchonga ulimi wake. Lakini, wazo la ulimi uliochongeka linamaanisha kuzungumza katika njia inayosababisha shida. Na wazo la nyoka kuwa na ulimi ulio chongeka inawakilisha ukweli kuwa nyoka wengi wana sumu.

Psalms 140:4

mikono ya waovu

nugu ya waovu

wameweka mtego ... sambaza wavu ... weka kitanzi

Aina bayana ya mitego sio muhumi kuliko wazo la kwamba"waovu ... watu wenye vurugu" wanapanga kusababisha shida kwa mwandishi wa zaburi.

Psalms 140:6

sikia vilio vyangu

Huu ni wito wa msaada. "nisikie ninapokuita sasa unisaidie"

unalinda kichwa changu katika siku ya vita

Kichwa cha mtu huwa kwenye hatari kubwa wakati wa vita. "unanilinda ninapoenda vitani"

vita

Hapa"vita" inaweza kumaanisha shida kubwa ya aina yoyote.

usitimize hamu za waovu

"tafadhali usiwaruhusu waovu kupata wanachotamani"

waovu

"watu waovu"

Psalms 140:9

wanainua vichwa vyao

Hii ni ishara ya kuwa na kiburi. "wana kiburi"

acha madhara ya midomo yao wenyewe iwafunike

Hili ni ombi kuwa Mungu atawafanya watenda maovu kuteseka kwa shida walizosababisha kwa maneno waliyosema.

madhara ya midomo yao wenyewe

Taabu walizosababisha wenyewe kwa yale waliyosema.

iwafunike

Basi, wazuie kusababisha shida zaidi.

Acha makaa ya moto yawadondokee; watupe katika moto

Picha ya moto inamaanisha adhabu kali kwa ajili ya waovu.

shimo lisilo na mwisho

Hii inaweza kumaanisha kuzimu, ulimwengu wa wafu.

watu wa ndimi

wale wanaozungumza uovu kuhusu wengine bila sababu.

salama katika nchi

"salama katika maisha haya"

na uovu umwinde mtu mwenye vurugu

Hapa uovu unazungumziwa kana kwamba ni mtu anayelipiza kisasi kwa mtu mwingine.

Psalms 140:12

atampa hukumu mhitaji

Hapa hukumu inazungumziwa kana kwamba ni kit kinachoweza kupewa kwa mtu. "Atatenda katika hali ya kuwasaidia wahitaji"

kwa jina lako

kwako

Psalms 141

Psalms 141:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

kulilia

"nakuomba msaada"

njoo upesi kwangu

Mwandishi wa zaburi anazungumza kana kwamba Yahwe ni mtu aliyehitaji kuja kutoka sehemu nyingine kumsaidia. "Njoo upesi kunisaidia"

Nisikie ninapokuita

"Tafadhali nisikie ninapokuita" au "Nakuomba unisikie ninapokuita"

Na maombi yangu yawe kama uvumba

"Na maombi yangu yakupendeze kama harufu nzuri ya uvumba unavyowapendeza watu"

maombi yangu

Mwandishi wa zaburi anataka Yahwe kupendeza naye kwa sababu anaomba na kwa sababu ya maneno ya ombi lake.

mikono yangu iliyoinuka

"mikono niliyoinua juu." Mikon iliyo inuka ni njia nyingine ya kusema maombi. Watu waliinua mikono yao walipoomba au kumsifu Yahwe.

iwe kama sadaka ya jioni

iwe kama mnyama aliyechomwa katika madhabahu jioni. Mwandishi anazungumza kana kwamba anataka Yahwe apendezwe naye kama anavyopendezwa na wanaoleta wanyama kwa ajili ya sadaka. Anataka Yahwe apendezwe kwa sababu mwandishi wa zaburi anaomba au kwa sababu ya maneno ya ombi lake.

Psalms 141:3

weka ulinzi juu ya mdomo wangu

Mwandishi wa zaburi anazungumza kana kwamba maneno maovu ni wafungwa wanaojaribu kutoroka kutoka mdomoni mwake. "tafadhali nisaidie nisiseme mambo yaliyo maovu"

weka ulinzi juu ya

"mwambie mtu alinde"

linda mlango wa midomo yangu

Mwandishi wa zaburi anazungumza kana kwamba maneno maovu ni wafungwa wanaojaribu kutoroka kutoka mdomoni mwake. "tafadhali nisaidie nisiseme mambo yaliyo maovu"

kushiriki katika vitendo vya dhambi

"kufanya vitendo vya dhambi"

vyakula vyao vitamu

"vyakula maalumu"

Psalms 141:5

anipige

Mwandishi anazungumza kana kwamba kukemewa ni kumpiga mtu kimwili. "nikemee" au "nipige ili nisikie anaponirekebisha"

itakuwa kama fadhili kwangu

"anaponipiga, nitajua kuwa yule anayenipiga ananitendea fadhila"

itakuwa kama mafuta kichwani kwangu

Maana zinazowezekana ni kwamba mwandishi wa zaburi anazungumza kana kwamba mtu anayemsahihisha anamwekea mafuta kichwani mwake 1) kumpa heshima. "anaponisahihisha, nitajua kuwa yule anayenisahihisha ananitendea jambo jema" au 2) kufanya kichwa chake kipate unafuu.

na kichwa changu kisikatae kukubali

Kichwa kinamwakilisha mtu. "na niikubali kwa furaha"

maombi yangu daima ni dhidi ya matendo yao ya uovu

Maneno "matendo ya uovu" ni njia nyingine ya kusema watu waliotenda hayo matendo maovu. "Huwa naomba kwamba Yahwe awazuie watu waovu kutenda mambo maovu"

Viongozi wao watatupwa chini

Maana zinazowezekana ni 1) "Mtu atawatupa viongozi wao chini" au 2) "Viongozi wao watawatupa chini."

genge

ardhi yenye mteremko wa ghafla

mifupa yetu imetawanywa

Maana zinazowezekana ni 1) "watu wametupa mifupa yetu pande tofauti" au 2) kama matokeo ya kuanguka katika genge. "miili yetu imevunjika na mifupa yetu imelala ovyo.

Psalms 141:8

macho yangu yako kwako

Macho yanawakilisha mtu mzima. "ninaangalia kuona utakachofanya" au "nategemea unisaidie"

nakukimbilia wewe

"ninakuomba unisaidie"

nafsi yangu

Nafsi ni njia nyingine ya kusema mtu mzima. "mimi"

mitego waliyoniwekea

Mwandishi anazungumzia kumdanganya mtu mzuri ili kwamba mtu mzuri atende dhambi au ili watu waovu wamshinde kana kwamba ilikuwa kuweka mtego kwa ajili ya mnyama. Neno "mitego" ni njia nyingine ya kusema watu wenyewe. "watu wanaotafuta njia za kumdhuru"

vitanzi ... mitego

Vitanzi humnasa mnyama kwa njia ya kama wakati mitego humnasa mnyama kwenye kachumba kado, mara nyingi kaliko undwa kwa chuma au mbao.

mitego ya watenda uovu

"mitego ambayo wanaotenda maovu wametega"

Acha waovu waanguke kwenye nyavu zao wenyewe

Mwandishi wa zaburi anawazungumzia watu waovu kuwadanganya watu wazuri kana kwamba wawindaji wanatega wanyama. "Acha waovu waanguke kwenye mitego ya nyavu waliyoandaa kunasa watu wengine" au " Acha vitu viovu walichopanga waovu kwa ajili ya wenye haki viwatokee waovu wenyewe"

Psalms 142

Psalms 142:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Maschili

Hii inaweza kumaanisha mtindo wa muziki.

pango

sehemu ya wazi chini ya ardhi yenye ukubwa wa kutosha watu kutembea

Ninalilia msaada kwa Yahwe ... Ninaomba kwa ajili ya fadhili za Yahwe

"Ninalilia na kuomba msaada kwa Yahwe kwa ajili ya fadhili zake"

kwa sauti yangu

"kwa kutumia sauti yangu"

Ninamwagwa kilio changu mbele yake ... namweleza shida zangu

"Ninamwaga kilio changu na shida zangu mbele yake"

Ninamwagwa kilio changu mbele yake

Mwandishi anazungumzia kumweleza Yahwe kwa nini ana huzuni kana kwamba anamwaga kimiminiko kutoka kwenye chombo. "Namwambia yote kuhusu kwa nini nina huzuni"

namweleza shida zangu

"namwambia kuhusu yote yanayonifanya kuwa na wasiwasi"

Psalms 142:3

roho yangu imedhoofika ndani yangu

"niko mnyonge" au "nimekata tamaa sana"

unafahamu njia yangu

"unafahamu njia nayopaswa kuchukua." Mwandishi anazungumza kana kwamba afanyacho mtu ni njia ambayo mtu amepitia. "unafahamu namna ninavyopaswa kuishi"

Katika njia nayopita wameficha mtego kwa ajili yangu

Mwandishi wa zaburi anazungumzia watu kutaka kumdhuru kana kwamba walikuwa wakijaribu kutega mnyama. "Wanafanya mipango ili chochote nitakachofanya wanidhuru"

maisha yangu

Hii ni njia nyingine ya kusema "mimi."

Nikakuita

Huu ni wito wa msaada. "nikuita wewe kwa ajili ya msaada"

fungu langu

Maana zinazowezekana ni 1)"ninachotaka" au 2) "ninachohitaji" au 3) "nilichonacho"

katika nchi ya walio hai

"wakati niko hai"

Psalms 142:6

Sikia wito wangu

Huu ni wito wa msaada. "Nisikilize ninapokuita kwa ajili ya msaada"

Nimeshushwa chini sana

Maana zinazowezekana ni 1) "mimi ni mhitaji sana" na 2) "mimi ni mnyonge sana."

Leta nafsi yangu kutoka gerezani

Hili ni ombi. "nitoe gerezani"

nitoe shukrani kwa jina lako

Neno "jina" ni njia nyingine ya kusema mtu. "kutoa shukrani kwako"

Psalms 143

Psalms 143:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

Sikia ombi langu

Maneno "ombi langu" ni njia nyingine ya kusema mtu anaye omba. "Nisikilie ninapoomba kwako" au "Kuwa tayari kufanya ninachokuomba kufanya"

nijibu

"tafadhali fanya ninachokuomba ufanye"

Usiingie hukumuni

"Tafadhali usinihukumu" au "Nakusihi usinihukumu"

mtumishi wako

Mwandishi anajizungumzia mwenyewe kana kwamba anamzungumzia mtu mwingine. "mimi"

machoni pako hakuna aliye na haki

"haufikiri kuwa yeyote ana haki"

Psalms 143:3

amefuatilia nafsi yangu

"amenifukuza akijaribu kunishika"

amenisukuma chini hadi ardhini

"ameniangamiza kabisa"

Roho yangu imezidiwa ndani yangu

"Mimi mnyonge" au "Nimekata tamaa kabisa"

moyo wangu umekata tamaa

"sina matumaini tena"

Psalms 143:5

Naitisha akilini

"Nafikiria"

mafanikio yako

"yote uliyotimiza" au "mambo yote makuu uliyotenda"

natawanya mikono yangu kwako katika maombi

"naomba kwako na mikono yangu ikiwa imenyanyuka pembeni yangu"

nafsi yangu ina kiu na wewe katika nchi iliyokauka

Mwandishi wa zaburi anazungumzia kutaka kuwa na Mungu kana kwamba yuko katika nchi iliyokauka na pia alikuwa karibu ya kufa kwa kiu. "ninataka kuwa na wewe kama mtu aliye katika nchi iliyokauka mwenye kiu sana anavyotaka maji"

nafsi yangu ina kiu na wewe

Mwandishi anatamani kumjua Yahwe. Mkazo wa hamu yake kumjua yahwe ni kama mtu aliye na kiu sana. "na shauku na wewe"

nafsi yangu

Nafsi ni njia nyingine ya kusema mtu.

nchi iliyokauka

Ardhi ambayo kila kitu kimekufa kwa sababu hakuna maji.

Sela

Hili linaweza kuwa neno la kimuziki linalowaongoza watu jinsi ya kuimba au kujecheza vyombo hapa. Tafsiri zingine huandika neno hili la Kihebrabia, na zingine haziliweki.

Psalms 143:7

roho yangu ni dhaifu

"mimi ni mnyonge" au "nimekata tamaa sana"

Usifiche uso wako kwangu

Hili ni ombi. "Nakuomba usijifiche kwangu" au "Tafadhali usijifiche kwangu"

Usifiche uso wako kwangu

Mwandishi anamzungumzia Yahwe kukataa kufanya kile ambacho mwandishi wa zaburi anaomba kana kwamba Yahwe alikuwa anakataa hata kumtazama. "Usikatae kunisikiliza" au "Tafadhali nisikilize"

Nitakuwa kama hao waendao shimoni

"Nitakuwa kama mtu mwingine tu aliyekufa"

Acha nisikie uaminifu wako wa agano

"Nisababishe kusikia uaminifu wako wa agano" au "Niambie uaminifu wako wa agano"

asubuhi

Maana zinazowezekana ni 1) asubuhi ni muda ambao watu wa wakati huo walidhani unafaa kuomba, au 2) "asubuhi kwa asubuhi," kila siku.

Nioneshe

"Niambie"

njia ninayopaswa kutembea

Mwandishi wa zaburi anazungumzia jinsi watu wanavyoishi kana kwamba ni njia ambayo wanatembea. "jinsi unavyotaka niishi"

kwa kuwa ninainua roho yangu kwako

Maana zinazowezekana ni 1) "ninaomba kwako" au 2) "ninaamini kuwa utaniongoza na kunilinda"

Psalms 143:9

Nakimbia kwako kujificha

Maana zinazowezekana ni 1) "Nakimbia kwako ili nijifiche" na 2) "Nakimbia kwako ili unifiche na kunilinda."

kufanya mapenzi yako

"kufanya unachotaka nifanye"

aniongoze katika nchi ya unyofu

Maana zinazowezekan ni 1) "nasaidie niishi kwa haki" au 2) "maisha yangu yawe huru na taabu"

nchi ya unyofu

Maana zinazowezekana ni 1) hii ni sititari ya kuishi maisha ya haki au 2) "nchi tambarare," sitiari ya maisha yasiyokuwa na taabu.

Psalms 143:11

kwa ajili ya jina lako

x

adui wa maisha yangu

"adui wanaotaka kuchukua maisha yangu"

Katika uaminifu wako wa agano wakate adui zangu

"Onesha uaminifu wako wa agano kwa kuwakata adui zangu"

adui wa maisha yangu

"adui wa nafsi yangu" au, kuchukua "maisha yangu" kama njia nyingine ya kusema "mimi", "adui zangu"

Psalms 144

Psalms 144:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

mwamba wangu

Maana zinazowezekana ni1) "yule ambaye ananiweka salama" au 2) "yule anayenipa nguvu"

anayefunza mikono yangu kwa ajili ya vita na vidole vyangu kwa mapambano

Maneno "mikono" na "vidole" zinamaana ya "mimi." "anayeniandaa kwa ajili ya vita" au ""anayeniandaa kwa ajili ya mapambano"

uaminifu wangu wa agano

"yule ambaye ananionesha uaminifu wa agano"

ngome yangu ... namkimbilia

Mwandishi wa zaburi anatumia sitiari kusisitiza kwamba Yahwe atamlinda.

mnara wangu wa juu

Daudi anamzungumzia Yahwe kana kwamba ni ngome inayomlinda dhidi ya mashambulizi. Yahwe ndiye anayemlinda Daudi na hatari.

ngao yangu

Daudi anamzungumzia Yahwe kana kwamba ni ngao inayomlinda askari. Yahwe ndiye anayemlinda Daudi dhidi ya hatari.

yule ambaye namkimbilia

Kwenda kwa Yahwe kunazungumziwa kama kumkimbilia. "yule ambaye ninaenda kwake kwa ajili ya ulinzi"

yule unayedhibiti mataifa chini yangu

"yule anayenisaidia kuyashinda mataifa mengine"

Psalms 144:3

Yahwe, mtu ni nini hadi unamtambua au mwanadamu hadi unamfikiria?

"Mwanadamu ni mdogo sana ukilinganisha na vingine vyote ulivyoumba hadi ninashangaa kwamba unamtambua na kumwaza"

mtu ... mwanadamu

maneno mawili yote yanamaanisha wanadamu

kama pumzi ... kama kivuli kipitacho

Mwandishi anawafananisha wanadamu na hivi vitu kuonesha jinsi maisha yao yalivyo mafupi.

Psalms 144:5

sababishe ... ije chini ... gusa ... ifanye ... Tuma ... uwatawanye ... piga ... warudishe

Haya maneno yanatakiwa kutafsiriwa kama maombi na sio amri kwa sababu mwandishi anatambua kuwa Mungu ni mkuu zaidi yake.

Sababisha anga izame

Maana zinazowezekana ni 1) pasua anga wazi au 2) kunja mbigu kama tawi la mti linavyojikunja mtu anapotembea juu yake au kama mtu anavyokunja upinde kabla ya kupiga mishale.

katika kuchanganyikiwa

"ili wasijue wawaze nini au wafanye nini"

Psalms 144:7

Nyosha mkono wako toka juu; niokoe na maji mengi

Daudi anazungumza kana kwamba Mungu alikuwa kwenye ardhi juu ya mafuriko na ana mikono ya kimwili ambayo angeweza kumvuta Daudi kutoka kwenye mafuriko. Mafuriko ni sitiari ya taabu zilizosababishwa na "wageni." "Unaweza kutenda, nisaidie nizishinde taabu zangu"

kutoka mkono wa wageni

Hapa "mkono" unaashiria nguvu."kutoka katika nguvu ya wageni"

Midomo yao inazungumza uongo

"Wanazungumza uongo"

mkono wao wa kuume ni uongo

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi anazungumzia utamaduni wa kuinua mkono wa kuume ili kuapa kuwa anachotaka kusema mtu mahakamani ni kweli, "wanadanganya hata wanapoapa kusema ukweli," au 2) "mkono wa kuume" ni sitiari ya nguvu, "kila kitu walichopata, wamepata kwa kusema uongo"

Psalms 144:9

wimbo mpya

Maana zinazowezekana ni 1) "wimbo ambao hakuna mtu amewahi kuimba" au 2) "wimbo ambao sijawahi kuimba"

kwako, unayewapa ...wafalme, uliyemwokoa

"kwako. Ni wewe unayewapa ... wafalme. Ni wewe ulimwokoa"

Daudi mtumishi wako

Daudi anajizungumzia kana kwamba ni mtu mwingine. "mimi, Daudi, mtumishi wako"

na upanga mwovu

Daudi anawazungumzia watu waovu kana kwamba ni upanga wanaotumia kama silaha. "kutoka kwa watu waovu waliokuwa wanajaribu kumuua"

Niokoe na uniweke huru

"Tafadhali niokoe na uniweke huru"

kutoka katika mkono wa wageni

Hapa "mkono" unaashiria nguvu."kutoka katika nguvu ya wageni"

Midomo yao inazungumza uongo

"Wanazungumza uongo"

mkono wao wa kuume ni uongo

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi anazungumzia utamaduni wa kuinua mkono wa kuume ili kuapa kuwa anachotaka kusema mtu mahakamani ni kweli, "wanadanganya hata wanapoapa kusema ukweli," au 2) "mkono wa kuume" ni sitiari ya nguvu, "kila kitu walichopata, wamepata kwa kusema uongo"

Psalms 144:12

kama mimea inayokuwa kikanilifu

yenye afya na imara

katika ujana wao

muda ambao watu wanakua

binti zetu kama nguzo za pembeni zilizochongeka

"na binti zetu wachongeke kama nguzo za pembeni"

nguzo za pembeni zilizochongeka

"nguzo nzuri zinazobeba pembe za nyumba kubwa"

nguzo za pembeni zilizochongeka, zenye umbo zuri kama za hekalu

"nguzo zilizochengeka kufanya hekalu lipendeze"

maelfu na elfukumi katika mashamba yetu

"maelfu—hata makumi elfu!—na wajaze mashamba yetu"

Psalms 144:14

Hakuna mtu atakayepasua kwenye kuta zetu

"Hakuna mtu atakayeweza kuvamia mji wetu"

wala kilio

"hakuna mtu atakayelia kwa maumivu" au "hakuna mtu kuomba omba chakula" au "hakuna tu kuita hukumu"

Psalms 145

Psalms 145:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

zaburi ya kusifu ya Daudi

"Hii ni zaburi ya kusifu ambayo Daudi aliandika"

Nitakutukuza wewe

"Nitawaambia watu jinsi ulivyo wa ajabu"

Nitabariki jina lako

Neno "jina" ni njia nyingine ya kusema Yahwe mwenyewe. "jina lake tukufu libarikiwe", "ubarikiwe" au "fanya kinachokufurahisha"

Nitalisifu jina lako

Neno "jina" ni njia nyingine ya kusema Yahwe mwenyewe. "nitakusifu" au "nitawaambia watu jinsi ulivyo mkuu"

Psalms 145:4

matendo yako makuu

"vitu unavyoweza kufanya kwa sababu una nguvu"

Psalms 145:6

nitatangaza wema wako uliojaa tele

"nitawaambia watu jinsi ulivyo mwema sana"

Psalms 145:8

umejaa tele uaminifu wa agano

Mwandishi anazungumzia uaminifu wa agano kana kwamba ni kitu cha kimwili ambacho mtu anaweza kumiliki kiasi kikubwa chake. "ni mwaminifu kabisa kwa agano lako"

rehema zake ziko juu ya kasi zake zote

"watu wanaweza kumwona akionesha huruma katika kila kitu afanyacho"

Psalms 145:10

Yote ulivyoumba vitakupa shukrani

"Watu wote uliowaumba watakupa shukrani" au "Itakuwa kana kwamba kila kitu ulichoumba kitakupa shukrani"

Psalms 145:13

unadumu katika vizazi vyote

"unabaki milele"

Psalms 145:14

anashikilia wote wanaoanguka ... anawainua wote walioinama

Mwandishi anamzungumzia Yahwe kuwatia moyo watu kana kwamba alikuwa akiwasaidia watu waliokuwa wandhaifu kimwili. "huwatia moyo wale walio kata tamaa"

Macho ya wote yanasubiri

"Kila mtu anasubiri"

Unafungua mkono wako

"Unatoa kwa ukarimu"

kuridhisha hamu za kila kiumbe hai

"unampa kila mtu zaidi ya anachohitaji na kiasi anachotaka"

Psalms 145:17

Yahwe ni wa haki katika njia zake zote

"Watu wanaweza kuona katika yote ambayo Yahwe anafanya kuwa yeye ni mwenye haki"

mwenye fadhili katika yote atendayo

"na ni mwenye fadhili katika yote atendayo" au "watu wanaweza kuona katika mambo yote ambayo Yahwe anafanya ya kuwa ni mwenye fadhili"

yuko karibu kwa wale wote wanaomwita

"anatenda upesi kuwasaidia wale wanaoomba"

wale wote wanaomwita kwa uaminifu

"kwa wale wanaosema ukweli tu wanapoomba" au "kwa wote wale anaowaamini wanapoomba"

Psalms 145:20

Mdomo wangu uta...

"Nita..."

utazungumza sifa za Yahwe

"Nitawaambia wote jinsi Yahwe alivyo mwema"

acha wanadamu wote wabariki jina lake

Neno "jina " njia nyingine ya kusema Yahwe mwenyewe. "jina lake tukufu libarikiwe," "acha watu wote wambariki" au "acha watu wote wafanye kinachomfurahisha"

Psalms 146

Psalms 146:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Msifu Yahwe, nafsi yangu

Hapa "nafsi" inawakilisha undani wa mwandishi. Mwandishi anajiamuru kumsifu Yahwe. "Nitamsifu Yahwe kwa nafsi yangu yote" au "Nitampa Yahwe sifa kwa maisha yangu yote"

kwa maisha yangu yote

"hadi nife" au "wakati ninaishi"

Psalms 146:3

kwa wana wa wafalme

Hapa "wana wa wafalme" inawakilishwa viongozi wote wanadamu.

kwa wanadamu, ambamo hakuna wokovu

"kwa mtu yeyote kwa sababu hawezi kukuokoa"

kwa wanadamu

"kwa watu"

Pumzi ya mtu inaposimama

Hii ni njia ya ustarabu ya kumaanisha mtu anakufa. "Mtu anapokufa"

anarudi mavumbini

Hii inamaanisha kamaMungu alivyomuumba binadamu wa kwanza, Adamu, kutoka mavumbini, hivyo pia mwili wa mtu utaoza na kuwa mavumbi tena atakapokufa.

Psalms 146:5

Yahwe ameumba mbingu na dunia

Maneno "mbingu" na "dunia" yanamaanisha kila kitu kilichopo ulimwenguni.

hufuata uaminifu

"hubaki mwaminifu"

Psalms 146:7

Anapitisha hukumu

"Anaamua mambo kwa usawa"

kwa waliokandamizwa

"kwa watu waliokandamizwa" au "kwa wale ambao watu wengine wamewakandamiza"

kwa wenye njaa

"kwa watu wenye njaa" au "kwa wale walio na njaa"

hufungua macho ya vipofu

Kumsababisha mtu kipofu kuona inazungumziwa kana kwamba Yahwe alikuwa anafungua macho yake. "husababisha vipofu kuona"

vipofu

"watu vipofu" au "wale walio vipofu"

Yahwe huwainua wale walioinama chini

Yahwe kumsaidia mtu inazungumziwa kana kwamba anamsaidia mtu kimwili kusimama. "Yahwe huwasaidia wale walio kata tamaa" au "Yahwe huwasaidia wale walio wanyonge"

walioinama chini

Hili ni tendo lenye ishara ya kukata tamaa na kuomboleza.

Psalms 146:9

huwainua

Mungu kumsaidia mtu kunazungumziwa kana kwamba alikuwa akiwanyanyua juu kimwili.

Mungu wako, Sayuni

Hapa "Sayuni" inawakilisha watu wote wa Israeli. Mwandishi anazungumza na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa hapo wakimsikiliza. "Mungu wenu, watu wa Israeli"

katika vizazi vyote

"atatawala katika vizazi vyote" au "atatawala milele"

Psalms 147

Psalms 147:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

ni vyema

"ni vyema kuimba sifa"

sifa inafaa

"sifa inastahili"

Psalms 147:2

Huwaponya waliovunjika moyo na kuziba vidonda vyao

Mwandishi anazungumzia huzuni ya watu na kukata tamaa kana kwamba ni vidonda vya kimwili, na Yahwe kuwatia moyo kana kwamba anaponya vidonda vyao. "Huwatia moyo wale walio na huzuni na kuwasaidia kupona na vidonda vyao vya kihisia"

Psalms 147:4

uelewa wake hauwezi kupimwa

"hakuna mtu anayeweza kupima uelewa wake" au "uelewa wake hauna mwisho"

Psalms 147:6

Yahwe huwainua waliokandamizwa

Mwandishi anazungumzia yahwe kuwapa heshima wale walio kandamizwa kana kwamba Yahwe alikuwa akiwainua kutoka ardhini. "Yahwe huwapa heshima walio kandamizwa"

huwaleta waovu chini ardhini

Mwandishi anamzungumzia Yahwe kuwaaibisha waovu kana kwamba Yahwe alikuwa akiwalazimisha kulala ardhini. "huwaaibisha waovu"

kwa kinubi

"huku wakicheza kinubi"

Psalms 147:8

na kwa wana wa kunguru wanapolia

"na huwapa chakula wana wa kunguru wanapolia"

wanapolia

"wanapoita"

Psalms 147:10

Hapendezwi na nguvu ya farasi

"Farasi wenye nguvu hawampendezi"

miguu yenye nguvu ya mtu

Maana zinazowezekana ni 1) "miguu yenye nguvu" ni njia nyingine inayowakilisha jinsi mtu anavyoweza kukimbia mbio. "watu wanaoweza kukimbia mbio" au 2) "miguu yenye nguvu" inawakilisha nguvu ya mtu mzima. "jinsi mtu alivyo na nguvu"

Psalms 147:12

Yerusalemu ... Sayuni

Mwandishi anazungumzana Yerusalemu, ambayo pia aniita Sayuni, kana kwamba ni mtu. Majina ya mji ni njia nyingine ya kuwaita watu wanaoishi humo. "watu wa Yerusalemu ... watu w Sayuni"

Kwa kuwa huimarisha vyuma vya malango yako

Msemo "vyuma vya malango yako" unawakilisha mji kwa ujumla. Yahwe ataifanya Yerusalemu kuwa salama kutoka kwa uvamizi wa adui. "Kwa kuwa huilinda Yerusalemu"

huwabariki ... miongoni mwenu

Mwandishi anawazungumzia wanaoishi Yerusalemu kana kwamba ni watoto wa Yerusalemu. "huwabariki wale wanaoishi Yerusalemu"

Huleta mafanikio

"Huleta amani." Maana zinazowezekana ni 1) Yahwe husababisha watu wanaoishi Yerusalemu kufanikiwa kwa mali na kwa fedha au 2) neno lililotafsiriwa kama "mafanikio" linamaanisha "amani" na Yahwe huitunza yerusalemu dhidi ya mashambulizi ya adui.

Psalms 147:15

amri yake inakimbia haraka sana

Mwandishi anaelezea amri za Mungu kana kwamba ni mjumbe anayekimbia haraka kufikisha ujumbe wa Mungu.

Huifanya theluji kama sufu, husambaza jalidi kama majivu

Hii inasisitiza jinsi ilivyo rahisi kwake kufanya hivi vitu. Hufunika ardhi kwa theluji kwa urahisi kama mtu anavyofunika kitu kwa blangeti wa sufu. Na huondoa jalidi kwa wepesi kama upepo unavyopuliza majivu.

Psalms 147:17

Huigawa mvua ya mawe kama makombo

Yahwe husambaza mvua ya mawe kwa wepesi kama mtu anavyosambaza chembechembe za mkate. "Huigawa mvua ya mawe kwa urahisi, kana kwamba ni makombo"

Huigawa

"Hutuma"

mvua ya mawe

mvua yenye vipande vidogo vya barafu kutoka angani

nani anawezakustahimili baridi anayoituma

Mwandishi anatumia swali hili kusisitiza kuwa ni vigumu kuvumilia hali ya hewa ya baridi ambayo Yahwe husababisha. "hakuna anayeweza kuishi katika baridi anayoituma"

Hutuma amri yake na kuyayeyusha

Mwandishi anazungumzia amri ya yahwe kana kwamba ilikuwa ni mjumbe wake. "Huamuru barafu kuyeyuka"

Psalms 147:19

Alitangaza neno lake kwa Yakobo, sheria zake na amri zake za haki kwa Israeli

Mistari hii miwili inamaana moja na inasisitiza kuwa Yahwe alitoa sheria yake kwa Israeli pekee.

sheria zake na amri zake za haki kwa Israeli

"Alitangaza sheria zake na amri zake za haki kwa Israeli"

sheria zake na amri zake za haki

Maneno "sheria" na "amri za haki" pamoja na "neno" katika mstari uliopita, yote yanamaanisha sheria ya Musa.

hawazijui

Mataifa mengine hayajui amri za Yahwe.

Psalms 148

Psalms 148:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Msifuni Yahwe, nyie mbinguni ... nyie mlio juu

"Msifuni Yahwe, nyie mbinguni ... nyie mlio angani." Mistari hii miwili ina usambamba. Msemo "juu" una maana sawa na "mbinguni" katika mstari uliopita"

Psalms 148:3

Msifuni, juana mwezi

Mwandishi anazungumza na jua na mwezi kana kwamba ni watu na anaziamuru kumsifu Yahwe. "Msifuni Yahwe, jua na mwezi, kama watu wafanyavyo"

msifuni, nyota zote zinazong'aa

Mwandishi anazungumza na nyota kana kwamba ni watu na anaziamuru kumsifu Yahwe. "Msifuni Yahwe, nyota wa kung'aa, kama watu wafanyavyo"

Msifuni, mbingu ya juu zaidi

Msemo "mbingu ya juu zaidi" ni lahaja ya kumaanisha mbingu yenyewe. Mwandishi anazungumza na mbingu kwan kwamba ni mtu na anaiamuru kumsifu Yahwe. "Msifu yahwe, mbingu iliyo juu zaidi, kama watu wafanyavyo"

nyie maji mlio juu ya anga

Mwandishi anazungumza na "maji mlio juu ya anga" kana kwamba ni watu na anayaamuru kumsifu Yahwe. "Msifuni Yahwe, maji mlio juu ya anga, kama watu wafanyavyo"

maji mlio juu ya anga

Mwandishi anazungumzia sehemu juu ya anga ambapo maji huhifadhiwa na mvua hutokea.

Psalms 148:5

Acha walisifu jina la Yahwe

Hapa neno "jina" linamwakilisha Yahwe mwenyewe. "Acha wamsifu Yahwe"

vikaumbwa

"aliviumba"

ametoa amri ambayo hatabadili

Maana zinazowezekana ni 1) "ametoa amri ambayo ni ya milele" au 2) "ametoa amri ambayo hawatakaidi"

ametoa

"kutoa" kama mfalme anavyotoa

Psalms 148:7

vilindi vyote vya bahari

Msemo huu unawakilisha kila kiumbe kinachoishi katika vilindi vya bahari. "viumbe vyote katika vilindi vya bahari"

moto na mvua ya mawe, theluji na mawingu, upepo wa dhoruba

Mwandishi anazungumza hivi vitu vya asili kana kwamba ni watu na kuviamuru kumsifu Yahwe.

upepo wa dhoruba unaotimiza neno lake

Msemo "neno lake" unawakilisha kile ambacho yahwe ameamuru. "upepo wa dhoruba unaofanya kile ambacho Yahwe ameamuru"

Psalms 148:9

Kauli Unganishi:

Mwandishi anaendelea kuzungumza na vitu ambavyo sio binadamu kana kwamba ni watu na kuviamuru kumsifu Yahwe.

wanyama pori na wakufugwa

"wanyama wote"

Psalms 148:11

Kauli Unganishi:

Mwandishi anawaamuru watu wote kumsifu Yahwe

mataifa yote

Neno "mataifa" linawakilisha watu wanoishi katika mataifa hayo. "watu wa mataifa yote"

vijana wanaume na wanawali, wazee na watoto

Mwandishi anatumia tofauti hizi za jinsia na umri kuwakilisha kila mtu.

Psalms 148:13

jina la Yahwe, kwa kuwa jina lake pekee

Hapa neno "jina" limwakilisha Yahwe mwenyewe. "Yahwe, kwa kuwa yeye pekee"

utukufu wake unasambaa juu ulimwengu na mbingu

Mwandishi anazungumzia ukuu wa Yahwe kama utukufu wake kuwa juu ya ulimwengu na mbingu.

Ameinua pembe za watu wake

Mwandishi anazungumzia nguvu kana kwamba ni pembe la mnyama. Kuinua pembe la mnyama ilikuwa ni ishara ilioshiria ushindi wa kijeshi. "Amewafanya watu wake kuwa na nguvu" au "Amewapa watu wake ushindi"

kwa ajili ya sifa kutoka kwa waaminifu wake wote

"ili kwamba waaminifu wake wote wamsifu"

watu karibu naye

Mwandishi anamzungumzia Yahwe kuwapenda watu wake kana kwamba watu wake wako karibu naye kimwili. "watu awapendao"

Psalms 149

Psalms 149:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi wa zaburi anazungumza na watu wote wa Mungu.

wimbo mpya

Maana zinazowezekana ni 1) "wimbo ambao hujawahi kuimba" au 2) wimbo ambao hakuna mtu aliyewahi kuimba.

imbeni sifa yake

"msifuni kwa nyimbo"

Psalms 149:2

ifurahi katika yeye aliyekuamba

Maana zinazowezekana ni 1) "furahi kwa sababu aliwaumba" au 2) "furahi kwa sababu aliyewaumba ni mwema."

wamfurahie mfalme wao

Maneno "mfalme wao" inawezekana kumaanisha Mungu. Maana zinazowezekana ni 1) "furahi kwa sababu ni mfalme wao" au 2) "furahi kwa sababu mfalme ni mwema."

wasifu jina lake

Neno "jina" ni njia nyingine ya kusema Yahwe mwenyewe. "msifuni yeye" au "waambie watu alivyo mkuu"

tari

chombo cha muziki chenye kichwa kama ngoma kinachoweza kugongwa na kina vipande vya chuma vimezunguka pembeni vinavyotoa sauti chombo kinapotikiswa.

Psalms 149:4

anawatukuza wanyenyekevu kwa wokovu

"anawapa utukufu wanyenyekevu kwa kuwaokoa kutoka kwa maadui zao"

vitandani mwao

"hata wanapolala chini kusinzia usiku"

Psalms 149:6

Sifa za Mungu ziwe kwenye midomo yao

Mdomo ni njianyingine ya kusema mtu mzima. "Daima wawe tayari kumsifu Mungu"

upanga wenye makali mawili mkononi mwao

upanga wenye makali mkononi mwao - Neno "upanga" ni njia nyingine ya kusema kuwa tayari kupigana vitani. "wawe tayari wakati wote kwenda vitani kwa ajili yake"

mataifa

Msemo "mataifa" ni njia nyingine ya kusema watu wanaoishi katika mataifa. "watu wa mataifa"

Psalms 149:8

minyororo

Hizi zinaundwa na vyuma vizito na zinazuia kusogea kwa mfungwa.

pingu

Kitu cha miduara miwili kilicho tengenezwa na chuma na mnyororo katikati yake zinazozuia kusogea kwa miguu au mikono ya mfungwa.

watatekeleza hukumu iliyoandikwa

kufanya kile ambacho Yahwe alimwambia Musa kuandika ili watu wafanye kwa wale wenye hati.

Psalms 150

Psalms 150:1

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Taarifa ya Jumla:

kuzingatia zaidi kusifu na kuabudu na jambo la kawaida hekaluni.

Msifuni Mungu katika mahali pake patakatifu

Hekalu la Mungu lilikuwa likijulikana zaida kama sehemu yake takatifu. Hii ilikuwa sehemu iliyotumika zaida kwenda kumwabudu Mungu.

matendo yake makuu

"mambo makubwa aliyotenda." "Matendo makubwa" ya Mungu yanaweza kumaanisha 1) ya asili kama radi na matetemeko au 2) miujiza kama uponyaji na ushindi mkubwa vitani.

Psalms 150:3

Taarifa ya Jumla:

Hiki kipande kinakazia kumsifu na kumwabudu Mungu kwa vyombo vya muziki na kucheza.

matari

Tari ni chombo cha muziki chenye kichwa kama ngoma kinachoweza kugongwa na kina vipande vya chuma vimezunguka pembeni vinavyotoa sauti chombo kinapotikiswa.

matoazi

sahani mbili nyembamba za chuma zinazogongwa pamoja kutengeneza sauti kubwa.

Psalms 150:6

Taarifa ya Jumla

Huu mstari ni zaidi ya mwisho wa zaburi hii. ni kauli ya kufunga kwa ajili ya kitabu chote cha 5 cha Zaburi, kinachoanzia Zaburi 107 na kuishia na Zaburi 150.

kila kitu kilicho na uhai

Maana zinazowezekana ni 1) watu wote walio hai wanapaswa kumsifu Mungu au 2) viumbe vyote vilivyo hai vinapaswa kumsifu Mungu.

Proverbs 1

Proverbs 1:1

Maelezo ya Jumla

Mstari wa 2-23 ni mashairi

kwa kufunza hekima na mafundisho

"kwa kukufunza jinsi ya kuwa na busara na kukuelekeza namna ya maisha kuishi kwa uadilifu.

kwa kufunza maneno ya ujuzi

"kwa kukusaidia kufahamu mafundisho ya busara"

ili kupokea

"ili tuweze kupokea"

ili kupokea mafundisho kwa ajili ya kuishi

" mpate kufunzwa namna ya kuishi"

Proverbs 1:4

pia ni kuwapa hekima wajinga

' pia kuwafunza wale ambao ni wajinga namna ya kuwa na busara"

wajinga

"bila uzoefu, isiyo kamavu/uchanga"

kuwapa maarifa na busara vijana

"na kuwafunza vijana wanachohitaji kufahamu na jinsi ya kutambua jambo zuri la kufanya"

busara

kufahamu kinachopaswa kufanyika katika mazingira husika.

Watu wenye busara wasikie na kuongeza elimu yao

"Wale wenye busara wazingatie na kujifunza zaidi"

watu wenye ufahamu wapate mwongozo

"watu wenye ufahamu wajifunze kwa methali hizi jinsi ya kufanya maamuzi mazuri"

vitendawili

misemo ambayo mtu anaweza kuifahamu baada tu ya kutafakari juu yake.

Proverbs 1:7

Maelezo ya Jumla

baba anamfundisha mtoto wake.

hofu ya Yahwe ni mwanzo wa maarifa

"Lazima umwogope Yahwe kwanza ili uanze kujua busara" au "lazima kumheshimu na kuwa na staha kwa Yahwe kwanza ili kujifunza busara"

Yahwe

Hili ni jina lake Mungu ambalo alilifunua kwa watu wake katika Agano la Kale.

wapumbavu hudharau hekima na mafundisho

"wale wasiothamini busara na maelekezo ni wapumbavu"

wala usijiweke kando

Hii ni nahau kumaanisha " usipuuzie" au " usikatae"

vitakuwa kilemba cha neema kwa ajili ya kichwa chako na mikufu yenye kuning'inia shingoni mwako

"yatakufanya uwe na busara kama kuvaa kilemba kwenye kichwa chako au mikufu kuzunguka shingo yako inavyokupendeza"

kilemba

duara iliyofumwa kwa majani au maua

mikufu

mapambo yanayovaliwa shingoni

Proverbs 1:10

wakijaribu kukushawisha kwenye dhambi zao

" jaribu kukuvuta kwenye dhambi wanazotenda"

kataa kuwafuata

usiwasikilize

kama watasema

mfano wa ushawishi wa wenye dhambi

tuvizie

kujificha na kusubiri muda muafaka

Proverbs 1:12

Maelezo ya Jumla

Mstari 12-14 ni mwisho wa kauli ya kihisia ya waovu ambao wanajaribu kuwashawishi wengine kufanya dhambi.

Tuwameze wangali hai, kama kuzimu inavyowachukua wale wenye afya

wenye dhambi wanaongea juu ya kuwaua watu wasio na hatia kama kuzimu ambavyo hupeleka chini kwa wafu watu wenye afya.

Tuwameze..., kama kuzimu inavyowachukua wale wenye afya

kaburi linafananishwa kama mtu ambaye huwameza wanadamu na kuwapeleka chini katika sehemu ya wafu.

kama kuzimu inavyowachukua wale wenye afya

waovu wanatarajia kuwaangamiza mateka wao kwa jinsi ile ile ambayo kuzimu(sehemu ya wafu) inavyowachukua hata watu wenye afya.

tuwafanye kama wale ambao huanguka kwenye shimo

"shimo" ni neno jingine lenye maana ya kuzimu au sehemu ambayo wafu huishi.

Tupa kura yako pamoja nasi

Hii ni nahau "jiunge nasi"

Sisi kwa pamoja tutakuwa na mkoba mmoja

"Mkoba" hapa unawakilisha kila kitu wanachoiba. "Sisi tutagawana kwa usawa kila kitu ambacho tumeiba"

mkoba

begi kwa ajili ya kubebea fadha

Proverbs 1:15

usiende katika njia ile pamoja nao; usiruhusu mguu wako kugusa ambapo wao hupita

kuepuka kuwa kwenye njia ya wenye dhambi" usiende pamoja na wenye dhambi au kutende matendo yao"

miguu yao hukimbilia maovu

"wapo tayari kutenda mambo maovu"

miguu yao hukimbilia

"miguu" inawakilisha mtu mwenyewe.

kumwaga damu

"damu" ni uzima wa mtu. Kumwaga damu ni kumuua mtu.

Kwa maana haifai kutandaza ... akiona

Hekima ya ndege ambao hujinasua na mitego wanayoiona inalinganishwa upumbavu wa wenye dhambi ambao hunaswa kwenye mitego ambayo hujitengenezea wenyewe.

Proverbs 1:18

Watu hawa huvizia ili kujiangamiza wenyewe- huweka mtego kwa ajili yao wenyewe

watu hujiangamiza wenyewe kwa mambo ya dhambi... ni kama hutega mtego kwa kujiangamiza wenyewe.

Hivyo ndivyo zilivyo njia za kila mmoja

"hivi ndivyo inavyotokea kwa kila mmoja"

mapato ya udhalimu huondoa maisha ya wale ambao huyashikilia

"mapato ya udhalimu yatawaharibu wale ambao hushushikamana nayo"

Proverbs 1:20

Maelezo ya Jumla

Katika 1:20-1:33 Hekima inaongelewa mithili ya mwanamke anayeongea na watu.

Hekima analia kwa sauti

"Hekima ni kama mwanamke ambaye hulia kwa sauti kuu"

hupaza sauti yake

Hii ni nahau "Huongea kwa sauti kuu"

katika viwanja

sehemu ambapo huweza kuwa na watu wengi. "kwenye soko" au "katika viunga vya mji"

kwenye kelele kuu za mitaa

sehemu ambapo mitaa yenye shughuli nyingi imeunganika au juu ya ukuta ambapo watu walioko kwenye kelele za mitaa wanaweza kuona na kusikia hekima ikiongea.

Hata lini, ninyi watu wajinga, mtapenda kuwa wajinga?

Hekima anatumia swali hili kuwakemea wasio na hekima. "Ninyi ambao ni wajinga lazima mkome kupenda kuwa wajinga"

wajinga

"bila uzoefu, isiyo komavu/uchanga"

Hata lini, ninyi wenye dhihaka, mtapenda dhihaka, na hata lini, ninyi wapumbavu, mtachukia maarifa?

Hekima anatumia swali hili kuwakema wenye dhihaka na wapumbavu. " Ninyi ambao hudhihaki lazima muache kupenda dhihaki, na ninyi wapumbavu lazima muache kuchukia maarifa"

Proverbs 1:23

Maelezo ya Jumla

Hekima anaendelea kuongea.

Sikiliza

"kusikiliza kwa umakini"

Mimi nitamimina mawazo yangu kwenu

Hekima anawaambia watu kila kitu anachofikiri juu yao, mawazo yake yanaongelewa mithili ya kimiminika ambacho anaweza kuwamiminia.

Mimi nitafanya maneno yangu yajulikane kwenu

" Nitawaambia yale ninayoyafikiria"

Mimi nimeunyosha mkono wangu

Hii ni nahau maana yake " Nimewaalikeni kuja kwangu"

Proverbs 1:26

Maelezo ya Jumla

Hekima anaendelea kuongea, akieleza ambacho hutokea kwa wale ambao humdharau.

Mimi nitacheka

kwa hiyo hekima ya mwanamke inawacheka kwa sababu wameipuuza.

katika msiba wenu

" mambo mabaya yanapotokea kwenu"

wakati hofu itakapo kuja

"wakati mtakapoogopa"

wakati hofu ya kuogopesha itakapokuja kama dhoruba... kama kisulisuli ... kuja juu yenu

mambo ya kutisha yatakayotekea kwa watu yanalinganishwa kama dhoruba itayowakumba na kusababisha hofu na maumivu.

kisulisuli

dhoruba ya upepo mkali ambao husababisha uharibifu

Proverbs 1:28

Sentensi Unganishi

Hekima anaendelea kuongea

Kisha wataniita

" Kisha wale ambao hunipuuza watanililia kwa msaada"

Kwa sababu wamechukia maarifa

Maarifa ni kujifunza."Kwa sababu wamekataa kujifunza ili wawe na busara"

hawakuchagua hofu ya Yahwe

" hawakumwogopa Yahwe" au "hawakumheshimu na kumtukuza Yahwe"

Hawakufuata maagizo yangu

"hawakuweza kukubali maagizo yangu" au " walikataa ushauri wangu"

Proverbs 1:31

Maelezo ya Jumla

mstari wa 33 unahitimisha kauli ya hekima ambayo ilianzia katika 1:20.

watakila matunda ya njia zao

"watapata madhara yanayotokana na matendo yao"

kwa matunda ya njama zao watashibishwa

"watateseka kwa mipango yao miovu"

wajinga

"bila uzoefu, isiyo kamavu/uchanga"

hufa wakati wanaporudi nyuma

"hufa kwa kuwa wanakataa kujifunza"

kutojali kwa wapumbavu kutawaangamiza

" wapumavu watakufa kwa sababu hawajali wanachopaswa kufanya"

kutojali

kukosa hamu juu ya jambo fulani

Proverbs 2

Proverbs 2:1

Maelezo ya Jumla

Baba anamfundisha mtoto wake kwa kutumia shairi.

kama utapokea maneno yangu

Hapa "maneno" yanawakilisha mafundisho " kama utasikiliza ambacho ninakufundisha"

kama utapokea

Huu ni mfululizo wa kauli zenye mashariti zinazofika tamati katika 2:5

zihifadhi amri zangu ndani yako

" zihesabu amri zangu kuwa za thamani kama hazina"

masikio yako yawe na usikivu kwa ajili ya hekima na kuelekeza moyo wako kwenye ufahamu

"kama masikio yako yatakuwa masikivu kwa ajili ya hekima na kuelekeza moy wako kwenye ufahamu"

masikio yako yawe na usikivu

"Jilazimishe kusikiliza kwa umakini wewe mwenyewe"

Hekima

"sikiliza mabo ya busara ambayo ninakufundisha"

elekeza moyo wako kwenye ufahamu

"jitahidi sana kufahamu maana ya busara"

Proverbs 2:3

Kama utalia kwa ajili ya ufahamu na kupaza sauti yako kwa ajili yake

'Kama utaweka umuhimu kumwomba Mungu na kumsihi kwa ajili ya ufahamu"

Kama utalia ... kama ukitafuta

Hizi ni kauli zenye amri, zingatia 2:1 na 1:1-2

paza sauti yako

Hii ni nahau, maana yake kuongea kwa sauti kuu au kupiga kelele.

kama utautafuta kama ambavyo ungetafuta fedha na kutafuta ufahamu kama ambayo ungetafuta hazini iliyositirika

kufanya bidii ili kujua maana ya busara.

kama utautafuata... kutafuta ufahamu

Kuwa na jitihada kuijua busara ni kama vile mtu ambavyo hutafuta vitu amabavyo ni vya lazima kwake.

utapata maarifa ya Mungu

kufanikiwa kumjua Mungu kunapewa picha ya kitu ambacho mtu hupata baada ya kutafuata.

Proverbs 2:6

kutoka katika kinywa huja maarifa na ufahamu

Hapa "kinywa" kinawakilisha Yahwe mwenyewe au Jambo ambalo anasema."Kutoka kwa Yahwe huja maarifa na ufahamu" au "Yahwe anatuambia sisi kile tunapaswa kukijua na kukifahamu"

Huhifadhi sauti ya hekima kwa ajili ya wale ambao humpendeza

Yahwe hufundisha kweli kwa wale ambao humpendeza.

kamili

yenye kutegemewa

yeye ni ngao kwa wale

Kwa kuwa Yahwe anauwezo wa kuwalinda watu wake anatajwa kama ngao.

ambao hutembea katika uadilifu

wanaoishi kama wanavyopaswa

huzilinda njia za mwenye haki

Mungu huwalinda wale ambao hutenda haki

atailinda njia yao

huwalinda wale ambao...

Proverbs 2:9

haki

adili

kila njia njema

kuishi katika njia ambao humpendeza Mungu.

hekima itaigia kwenye moyo wako

Hapa "moyo" unamaanisha utu wa ndani wa mwanadamu. "utajifunza namna ya kuwa na busara ya kweli"

yatakupendeza nafsi yako

"yatakupa furaha"

Proverbs 2:11

Busara Itakulinda, ufahamu utakuongoza

"kwa sababu unafikiri kwa kutafakari na kuifahamu kweli na ubaya utakuwa salama"

Busara

hali ya kuwa makini katika matendo na maongezi

atakulinda

kuongoza, kukinga au kumjali mtu au kitu

Vitakuokoa kutoka katika njia ya uovu

utajua kuishi mbali na yale maovu

kutoka katika njia ya uovu

uovu unaongelewa kama kwamba ni njia ya kupita mtu

ambao huziacha njia za haki na kutembea katika njia za giza

mtu anapoacha kutenda haki lakini huamua kutenda uovu ni kama mtu anayeacha kutembea kwenye njia sahihi na kuchagua kutembea kwenye njia ya giza.

ambao huacha

Hapa neno "ambao" linahusu watu wenye kuongea mambo ya kupotosha.

Proverbs 2:14

Hufurahia

hawa ni watu waliotajwa katika 2:11

hufurahia katika upotevu wa uovu

wanafurahi kutenda mambo ambayo wanajua ni maovu

Hufuata njia za udanganyifu

huwadanganya watu wengine

na hutumia udanganyifu huficha mapito yao

na hudanganga ili mtu yeyote isifahamu jambo walilofanya

Proverbs 2:16

Maelezo ya Jumla

Baba anaendelea kumfundisha mtoto wake jinsi ambavyo hekima itamlinda.

Hekima na busara vitakuokoa

"kama utakuwa na hekima na busara, utajiokoa wewe mwenyewe"

mwenza wa ujana wake

mume wake, ambaye aliyemwoa tangu ujanani

agano la Mungu wake

agano la ndoa ambalo amelifanya na mume wake katika uwepo wa Mungu.

Proverbs 2:18

nyumba yake inaelekea mauti

kwenda kwenye nyumba yake husanabisha mauti au njia ya kwenda nyumbani kwake ni njia ya kuelekea katika mauti.

mapito yake yatakuongoza

njia za kwenda kwenye nyumba yake zitakuongoza au namna ya anavyoishi itakuongoza.

kwa wale waliopo kwenye kaburi

roho za watu wafu, ni picha ya sehemu ya wafu

huingia kwake

kwenda kwenye nyumba yake na kulala pamoja naye, kama ambayo mtu anavyo lala na malaya.

hatazifikia njia za uzima

hawataishi maisha ya furaha tena au hawataweza kurudi katika nchi ya watu wenye uhai

Proverbs 2:20

kwa hiyo

mwandishi anasema faida za kupata ufahamu na busara

utatembea katika njia... fuata njia

utaishi katika njia... kufuata mfano

waovu wataondolewa kutoka katika nchi

"Yahwe atawaondoa waovu kutoka katika nchi"

waovu... wasioamini

"wale ambao ni waovu ... wale wasiokuwa na imani" au "watu waovu ... watu wasioamini"

wasioamini wataondolewa katika nchi

ambao hawaamini atawaondoa katika nchi

Proverbs 3

Proverbs 3:1

Maelezo ya Jumla

Mwandishi anaongea kama baba akimfundisha mtoto wake kwa kutumia shairi.

usizisahau amri zangu

"usiyasahau niyokuagiza"

yatunze mafundisho yangu ndani ya moyo wako

"Nilichokufundisha ukikumbuke daima"

wingi wa siku na miaka ya uzima

utaishi maisha marefu

Proverbs 3:3

usiruhu agano la uadilifu na uaminifu viondoke kwako

Hakikisha unatekeleza agano la uadilifu na uaminifu daima.

uyafunge pamoja kwenye shingo yako

uoneshe kwa furaha kama mtu ambovyo huvaa mikufu shingoni

yaandika kwenye kibao cha moyo wako

daima uyakumbuke kana kwamba umeyaandika kwenye kibao cha kudumu

katika upeo wa Mungu na wanadamu

katika hukumu ya Mungu na wanadamu

Proverbs 3:5

kwa moyo wako wote

" mambo yako yote"

usitegemee ufahamu wako mwenyewe

usiweke tumaini katika ufahamu wako wenyewe

katika njia zako zote

"katika kila jambo ulifanyalo"

yeye atazinyosha njia zako

atakupa mafanikia

Proverbs 3:7

usiw wenye busara katika macho yako mwenyewe

"usiwe wenye busara katika mawazo yako mwenyewe"

geuka mbali kutoka katika uovu

"usitende uovu"

itakuwa uponyaji katika mwilini mwako

"kama utafanya hivi, itakuwa uponyaji kwa ajili ya mwili wako"

Proverbs 3:9

ulivyozalisha

"kuvuna"

ghala zako zitajazwa

"ghala zako zitajaa"

ghala

majengo au chumba ambapo chakila huhifadhiwa

mashikizo yako yatapasuka

vifaa vyako vya kutunzia vitajaa kupita kawaida, kama vinakaribia kupasuka.

Proverbs 3:11

Maelezo ya Jumla

Mwandishi anaandika kama baba akimfundisha mwanawe.

mwana ambaye humpendeza

baba huonesha upendo kwa mwanae

Proverbs 3:13

mtu ambaye hujipatia hekima

mtu anayepata hekima

mbadala ambao fedha itakupa

faida ya biashara au uwekezaji

Proverbs 3:15

Maelezo ya Jumla

Mwandishi anaongea juu y hekima kama vile anaongea na mwanamke.

thamani

"a gharama" au "ghari"

ni mwenye wingi wa siku katika mkono wake wa kulia; katika mkono wake wa kushoto ni utajiri na heshima

hekima humpa mtu siku nyingi na utajiri na heshima

wingi wa siku

Hii nahau maana yake"maisha marefu"

Proverbs 3:17

Njia zake ni njia za upole na mapito yake yote ni amani

Hekima inatakutendea kwa upole na kukupa amani daima

Yeye ni mti wa uzima kwao ambao humshikilia

Hekima ni kama mti ambao huhifadhi uzima kwao ambao hula matunda yake

mti wa uzima

mti unaota uzima au mti ambao matunda yake hudumisha uzima

kwao ambao humshikilia

wao ambao hushikilia kwenye matunda yake

Proverbs 3:19

Yahwe aliumba dunia... aliziimarisha mbingu

Yahwe aliumba dunia.. aliziunda mbingu

vina hufunguka wazi

alisababisha mito kutiririka au alisababisha kuwepo kwa bahari

umande

maji ambayo hutokea ardhini wakati wa usiku

Proverbs 3:21

usiyapoteze kwenye upeo

usiyasahau

Yatakuwa uzima nafsini mwako

yatakuwa uzima kwa ajili yako

urembo wa kuvutia wa kuvaa shingoni mwako

kuonekana unavutia kama mtu ambavyo hujiremba mwenyewe kwa mikufu ya shingoni

urembo wa kuvutia

urembo ambao huonyesha kibali cha Yahwe

Proverbs 3:23

utatembea kwenye njia yako kwa usalama

maisha yako utaishi kwa usalama

mguu wako hautajikwaa

hutafanya mambo yenye makosa

wakati wa kulala

wakati unaposhuka kulala

usingizi wako utakuwa mtamu

usingizi wako utakuwa mzuri au utalala kwa amani

Proverbs 3:25

uharibidu wa waovu, wakati unapokuja

"Wakati waovu wanaposababisha uharibifu"

Yahwe atakuwa upande wako

Yahwe atakusaidia na kukutetea

ataulinda mguu wako usinaswe katika mtego

atakulinda na wale ambao wanataka kukudhuru

Proverbs 3:27

usizuie mazuri

"usizuie vitu vizuri" au "usizuie matendo mema"

wakati yapo katika uwezo wako kuyatenda

" wakati unao uwezo wa kusaidia"

unapokuwa na pesa

mtu anapokuwa na uwezo wa kusaidia leo, bali akamwambia jirani yake rudi tena keshao. "unapokuwa na pesa kwa wakati huu"

Proverbs 3:29

jirani

kwa kawaida ni mtu anayeishi jirani, au ambaye anayeishi katika jumuiya au kundi la watu wenye kufahamiana.

anayekuamini, mwaminifu

mtu mkweli na kutumainiwa

Proverbs 3:31

... wala usicahague moja ya njia zake

"usichague kuiga njia yake yoyote"

mtu mjanja ni chukizo kwa Yahwe

"Yahwe humchukia mtu mjanja"

mtu mjanja

mtu wenye dharau au mdanganyifu

mtu mwaminifu humpeleka katika ujasiri

"Yahwe ni rafiki wa karibu kwa waaminifu"

Proverbs 3:33

Laan ya Yahwe ipo juu ya mtu mwovu

"Yahwe ameilaani familia ya mtu mwovu"

Huibariki maskani ya watu wema

"huzibariki familia za watu wema"

huwapa fadhila watu wanyenyekevu

"huonyesha fadhila kwa watu wanyenyekevu" au "ni mkarimu kwa watu wanyenyekevu"

Proverbs 3:35

watu wenye busara hurithi heshima

"Watu wenye busara watapata heshima ya sifa njema"

wapumbavu watainuliwa kwa aibu yao

"Yahwe atamfanya kila mtu aone aibu ya wapumbavu"

Proverbs 4

Proverbs 4:1

Maelezo ya Jumla

Mwandishi ananena kama baba anayewafundisha watoto wake.

Sikiliza

"kusikiliza kwa umakini"

utajua maana ya ufahamu

"utajua jinsi ya kufahamu" au "utapata ufahamu"

Mimi ninakupa maagizo mazuri

"Ninachokufundisha mimi ni kizuri"

Proverbs 4:3

Mimi nilipokuwa mwana kwa baba yangu

"Mimi nilipokuwa bado mvulana nikijifunza kwa baba yangu"

mpole na mtoto pekee

"mtoto mpole wa pekee"

moyo wako uyazingatie maneno yangu

"Ukumbuke daima yale ambayo ninakufundisha"

Proverbs 4:5

Maelezo ya Jumla

Baba anaendelea kuwafundisha watoto wake mambo ambayo yeye alifundishwa na baba yake

Jipatie hekima

"fanya bidii kupata hekima kwa ajili yako mwenyewe" au "pata hekima"

usiyasahau

"yakumbuke"

usiyakatae

"kubali"

maneno ya kinwa changu

"yale ninayonena"

usimwache hekima na naye atakulinda; mpende na yeye atakuweka salama

Mwandishi ananena juu ya hekima kama mwanamke ambaye humlinda mtu ambaye ni mwaminifu.

usimwache hekima

" ishikilie kwa nguvu kabisa hekima"au " uwe mwaminifu kwa hekima"

mpende

" mpende hekima"

Proverbs 4:7

Maelezo ya Jumla

Baba anamalizia kuwafundisha watoto wake yale ambayo alifunzwa na baba yake.

tumia mapata yako yote kujipatia ufahamu

"thamini ufahamu zaidi kuliko yote unayoyamiliki"

mtunze hekima na yeye atakutukuza

"kama utamlea hekima, atakupa heshima kubwa"

mtunze

kujihisi au kuonyesha upendo mkuu kwamtu au kitu

atakuheshimu endapo utamkumbatia

"kama utapenda sana hekima, hekima itasababisha watu wakuheshimu"

ataweka kilemba cha heshima juu ya kichwa chako

"Hekima itakuwa kama kilemba juu ya kichwa chako ambacho huonesha heshima kuu"

Kilemba

duara iliyofumwa kwa majani au maua

atakupatia taji zuri

" hekima ni kama taji zuri juu ya kichwa chako"

Proverbs 4:10

na uyasikilize maneno yangu

"sikiliza kwa kuzingatia ninachokufundisha"

utakuwa na miaka mingi ya maisha yako

"utaishi miaka mingi"

Nianakulekeza katika njia ya hekima; Mimi ninakuongoza kwenye njia nyoofu

"niakufundisha jinsi ya kuishi kwa busara; ninafafanua njia njema ya kuishi"

unapotembea, hapana mtu atakayesimama katika njia yako na kama ukikimbia, hutajikwaa

"unapopanga kitu, utafanikiwa kukitekeleza"

Proverbs 4:13

shika maagizo, usiyaache yaondoke

"endelea kutii yale niyokufundisha na usiyasahau"

maana ni uzima wako

"maana yatautunza uzima wako"

usiifuate njia ya waovu na usienende kwenye njia ya wale watendao maovu

"usifanye yale wanayofanya watu waovu na usijiunge katika matendo ya watu watendao ubaya"

Jiepushe nayo

"iepuke njia ya waovu"

Proverbs 4:16

hawezi kulala hadi watende ubaya

watu waovu hutamani kutenda matendo mabaya

wameporwa usingizi wao

"hawawezi kulala"

hadi wamwangushe mtu

"mpaka wadhuru mtu"

wanakula mkate wa uovu na kunywa mvinyo wa vurugu

"wanakula mkate ambao wanaupata kwa kutenda mambo maovu na kunywa mvinyo ambao wanaupata kwa njia ya vurugu"

Proverbs 4:18

njia ya watu wenye haki ... njia ya waovu

"mwenendo wa watu wenye haki ...mwenendo wa waovu"

njia ya watu wenye haki ni kama nuru ya awali ambayo huzidi kung'ara

"watu wenye haki hutembea kwenye njia yao kwa salama kwa kuwa jua la asubuhi huangaza juu yake na wanga hung'aa zaidi

nuru ya awali

Hii ni mapambazuko au mawio

hadi mchana mkamilifu

"mpaka jua ling'are kwa wangavu zaidi" au "hadi mchana haswa"

njia ya waovu ni kama giza

"watu waovu hutembea kwenye hatari maana njia yao haina mwanga kuwawezesha kuona"

hawajua ambapo hujikwaa

"hawajua kwa nini hukumbwa na madhara na bahati mbaya"

Proverbs 4:20

sikiliza

"kusikiliza kwa umakini"

tega sikio lako kwenye kauli zangu

"sikiliza kwa usikivu kwa mambo amabyo ninakuambia"

usiache ziondoke kutoka machoni pako

"usiache kuzitafakari "

uzihifadhi moyoni mwako

"uzikumbuke daima"

Proverbs 4:22

maneno yangu ni uzima

"maneno yangu yanaleta uzima"

kwa wale wanaozipata

"kwa wale wanaozifahamu na kuzitenda"

afya katika mwili wao wote

"maneno yangu yataleta afya katika mwili wote kwa wale wanaoyapata"

utunze moyo wako salama na kuulinda

"tunza akili yako salama na kuyalinda mawazo yako"

kwa bidii yote

"kwa uthabiti na nguvu"

kutoka kwenye moyo wako hububujika chemchemi za uzima

"kila kitu unachosema huja kutoka katika mawazo yako" au "mawazo yako hubainisha mwenendo wa maisha yako"

Proverbs 4:24

weka mbali nawe maongezi ya ukaidi na weka mbali mazungumzo ya ufisadi

"usiongope na kusema kwa udanyanyifu"

macho yako yatazame mbele na ukaza mtazamo mbele sawasawa

"utazame mbele daima na ukaze mtazamo wako mbele moja kwa moja"

Proverbs 4:26

sawazisha njia kwa ajili ya mguu wako

"Tayarisha vizuri yale unayotaka kuyafanya"

sawazisha njia

"njia laini au "njia tulivu"

kisha njia zako zote zitakuwa salama

"kisha kila kitu unachofanya kitakuwa sawa"

usigeuke upande wa kulia au wa kushoto

"tembea wima kwenda mbele wala usiiache njia iliyo sawa"

ondoa mguu wako kwenye maovu

"kaa mbali na maovu" au "ondoka kwenye maovu"

Proverbs 5

Proverbs 5:1

Maelezo ya Jumla

Mwandishi ananena kama baba anayewafundisha watoto wake.

tega masikio yako

"sikiliza kwa makini"

busara

angalia 1:4

midomo yako iyalinde maarifa

"utaongea ambacho ni ukweli tu"

Proverbs 5:3

midomo ya malaya hutona asali

"maneno ya malaya ni matamu, kana kwamba hutona asali" au "busu la malaya ni tamu, kana kwamba midomo yake hutona asali"

kinywa chake ni laini kuliko mafuta

"kauli yake inashawishi na laini kuliko mafuta ya mizeituni" au "busu lake ni laini kuliko mafuta ya mizeituni"

lakini mwisho ni mchungu kuliko pakanga

"lakini mwishoni ni mchungu kama radha ya pakanga na atasababisha madhara"

pakanga

mmea ambao unaradha ya uchungu

hukata kama upanga wenye makali

"humjeruhi mtu, kama unavyojeruhi upanga mkali"

Proverbs 5:5

miguu yake huelekea chini kwenye mauti

"miguu yake" hapa anaongelewa mtu malaya. "Anatembea katika njia ambayo inaeleke kwenye mauti" au "mwenendo wake huelekea kwenye mauti"

hatua zake huelekea kwenye njia ya kuzimu

"hutembea katika njia ya kuzimu"au " tabia yake humpeleka kwenye njia ya kuzimu"

yeye haifikirii njia ya uzima

"hajali kuhusu mwenendo wa kumwongoza katika uzima"

hatua za mguu wake hutanga tanga

"hutembea katika njia ovu" au "hutanga tanga kana kwamba amepotea"

Proverbs 5:7

Sasa

Hapa walimu anaondoka katika hali na kuonya juu ya umalaya na kuanza kutoa ushauri.

nisikilize... usiache kusikiliza

sikiliza

usiache kusikiliza

"usikome kusikiliza"

maneno ya kinywa changu

"maneno yangu"

njia yako iweke mbali naye

"kaa mbali naye"

usiukaribie mlango wa nyumba yake

"usiende karibu na mlango wa nyumba yake" au " hata usisogee karibu na nyumba yake"

Proverbs 5:9

katika njia hiyo

inahusu njia aliyoizungumzia hapo mwanzo

hutatoa heshima yako kwa wengine

"isipoteze heshima yako nzuri miongoni mwa watu wengine" au "usipoteze utajiri wako kuwapa watu wengine"

au miaka ya uzima wako kwa mtu mkatili

"au kumpati mtu makatili uzima wako" au "kusababisha mtu mkatili akuue ungali bado kijana"

mtu mkatili

pengine huyu ni mume wa mke malaya, ambayo atamshughulikia kwa ukatili mtu anayelala na mke wake

wageni hawatasherekea kwa utajiri wako

"wageni wasikuchukulie utajiri wako wote"

kazi yako uliyofanya isiende katika nyumba ya wageni

"vitu ulivyopata visimalizike kwa kuishia kwenye famila za wageni"

Proverbs 5:11

nyama yako na mwili wako vikateketea

"mwili wako ukapotelea mbali" au "ukapotea"

vikateketea

"kuchoka kimwili" au "kuwa dhaifu na afya mbaya"

Mimi nilichukia mafundisho ... moyo wangu ulidharau kusahihishwa

huyu mtu alichukia alichoambiwa na walimu wake

jinsi gani nilichukia mafundisho

"nilichukia sana wakati mtu aliponielekeza"

moyo wangu ulidharau masahihisho

"Niliwadharau watu waliponionya"

Proverbs 5:13

kutega masikio yangu kwa walimu wangu

'"kuwasikiliza wale walionielekeza"

katikati ya kusanyiko, miongoni mwa watu waliokusanyika

jumuiya ilikusanyika ama kumwabudu Mungu au kuhukumu dhidi ya makosa yake.

Proverbs 5:15

maji kutoka katika birika lako mwenyewe ... maji yanayotiririka kutoka kwenye kisima chako mwenyewe

Mwandishi anazunguza juu ya mume kulala na mke wake pekee kana kwamba ni kunywa maji kutoka kwenye kisima au birika lake mwenyewe.

maji yanayotiririka

"maji mapya" au "maji ya kutiririka"

yapasa chemchemi zako ... miferji yako ya maji itiririke katika njia kuu?

"Chemchemi yako haipaswi ...mifereji yako ya majiji haipaswi kutiririka katika njia kuu"

njia kuu

maeneo ya wazi katika jiji au mjini ambapo miji miwili au zaidi inapokutana. Sehemu ya kawaida watu kukutana na kuongea.

Yawe

hii nahusu chemchemi na mifereji ya maji

wala si kwa ajili ya wageni pamoja nawe

"usichangie na wageni"

Proverbs 5:18

Chemchemi yako na ibarikiwe

"uweze kufurahia daima pamoja na mke wako"

mke wa ujana wako

"mwanamke ambaye ulimwoa wakati ukiwa kijana" au "mke wako kijana"

Ni ayala apendaye na kulungu mwenye madaha

"Ni mwanamke mzuri na mwenye kependeza kama ayala au kulungu"

mwenye madaha

"mzuri wakati apotembea"

maziwa yake yakutosheleze

"maziwa yake yakujaze furaha kama maziwa ya mama yanavyowatosheleza watoto wake kwa chakula"

daima akuleweshe kwa upendo wake

'upendo wake na ukutawale kama pombe inavyomtawala mlevi"

kwa upendo wake

kwa upendo wake kwako

Proverbs 5:20

Mwanangu, kwa nini wewe, uwe mateka wa malaya; kwa nini kuyakumbatia maziwa ya mwanamke asiye mwadilifu?

"Mwanangu, usitekwe na malaya!Usikumbatie maziwa mwanamke asiye mwadilifu!"

uwe mateka wa malaya

"kuruhusu malaya kukuteka wewe"

huona kila jambo... huzitazama njia zote

Mungu anafahamu kila jambo analolifanya kila mtu

njia zote anazochukia

"kila sehemu anapokwenda" au "kila kitu anachofanya"

Proverbs 5:22

mtu mwovu atatekwa kwa makosa yake mwenyewe

"mtu mwovu hataweza kuepuka madhara ya makosa yake"

nyuzi za dhambi yake zitamshika kwa nguvu

"kwa sababu ya dhambi zake, atakuwa kama mnyama aliyenaswa katika mtego"

upumabavu wake mkuu utampoteza

"upumbavu wake mkuu utamwongoza upotevuni"

upumabavu wake

"kwa sababu ya upumabavu wake"

Proverbs 6

Proverbs 6:1

weka pesa zako

tunza sehemu ya pesa zako

mdhamana kwa ajili ya mkopo wa jirani yako

maana: jirani yako anaweza kuja kwako kwa ajili ya kukopa au jirani yako anataka mkopo kwa mtu mwingine, lakini unaahidi kumlipa mkopesahaji kama jirani yako hataweza.

jirani

maana nyingine ni "rafiki"

umeweka mtego kwa ajili yako mwenyewe

"umetengeneza mtego ambao utakunasa wewe mwenyewe"

maneno ya kinwa chako

"ulichosema" au "ulichoahidi kufanya"

Proverbs 6:3

jiokoe mwenyewe

jilinde mwenyewe" au "jisaidie mwenye kutoka katika matatizo haya"

umeangukia kwenye mkono wa jirani yako

"jirani yako anaweza kuleta madhara kwako kama akitaka" au "jirani yako ananguvu juu yako"

jirani

"rafiki"

Proverbs 6:4

Macho yako usiyape usingizi na kope kope za macho yako kusinzia

"kaa macho, na kufanya unachoweza"

macho yako... kope zako

" mwenyewe"

jiokowe mwenyewe kama swala kutoka kwenye mkono wa mwindaji

"Epa kutoka kwa jirani yako kama swala ambaye hukimbia kutoka kwa mwindaji"

swali

Huyu ni mnyama ambaye hula majani na mara nyingi watu humwinda kwa ajili ya nyama. Mnyama huyu ni maarufu kwa kwa kukimbia mbbali upesi

kutoka kwenye mkono wa mwindaji

"kutoka kwenye udhibiti wa mwindaji"

kama ndege kutoka kwenye mkono wa mwindaji wa ndege

"epa kama ndege ambaye huruka kwenda mbali kutoka kwa mwindaji wa ndege"

Proverbs 6:6

Mtazame...zitafakari

"jifunze ...fikiri juu yake" au "cunguza kwa umakini... tafakari"

chungu

ni mdudu mdogo ambaye huishi ardhini au kichuguu anachojenga mwenyewe. Huishi katika makundi ya maelfu, na wanaweza kunyanyua viti vikubwa kuliko wenyewe.

zitafakari njia zake

"tafakari jinsi chungu anavyotenda"

kamanda, ofisa, au mtawala

Haya ni maneno yenye maana moja kusisitiza kuwa hakuna mtu mwenye mamlaka rasmi juu ya chungu .

huandaa chakula chake wakati wa jua... wakati wa mavuno huhifadhi chkula chake

Hapa inaonesha ni jinsi gani chungu huwajibika

wakati wa jua

ni majira ambapo baadhi ya miti huzaa matunda

Proverbs 6:9

Je utalala hata lini ... lini utainuka kutoka kwenye usingizi?

"Amka, wewe mtu mzembe! Inuka kwenye kitanda chako"

Usingizi kidogo ... mikono kujipumzisha

Haya ni aina ya mambo amabayo watu wazembe husema

Lala kidogo, sinzia kidogo

"nitaendelea kulala zaidi"

kukunja mikono kwa kujipumzisha

"nitakunja mikono yangu kwa utaulivu na kupumzika kidogo"

na umasikini wako utakuja

"ukiendelea kuwa mzembe, umasikini wako utakuja" au " Wakati umelala, umasikini utakuja"

umasikini wako utakuja kama mnyang'anyi

ghafula utakuwa masikini, kana kwamba mnyang'anyi amekuja na kukuibia kila kitu ulichonacho"

na uhitaji wako kama askari mwenye silaha

"na utakuwa mhitaji kana kwamba askari mwenye silaha amekuibia vitu vyako vyote"

askari mwenye silaha

"askari ambaye ameshikilia silaha" au "mtu mwenye silaha"

Proverbs 6:12

Mtu asyefaa...mtu mwovu

inasisitiza juu ya ubaya wa huyu mtu "mtu asiyekuwa na thamani-mtu mwovu"

huishi kwa udanganyifu wa kauli zake

"husema uongo daima"

hukonyeza macho yake, akifanya viashiria kwa miguu yake na kusonta kwa vidole vyake

Hii ni vile mtu mwovu huwasiliana kwa siri ili kudanganya watu wengine.

hukonyeza macho yake

mtu akikonyeza hufumba jicho moja kwa muda mfupi kama kiashiria cha siri kwa mtu mwingine.

Proverbs 6:14

Hutunga uovu

"huandaa ubaya" au "Hujitayarisha kufanya matendo mabaya"

kuchochea mafarakano daima

"Siku zote husababisha kutoelewana" au " hutafuta mafarakano daima na kuyaendeleza"

Kwa hiyo

"kwa sababu hiyo"

msiba wake utamkuta kwa ghafula

"msiba wake utamkamata"

msiba wake

hii inahusu msiba utakaotokea ambao mhusika ameusababisha.

ghafla; kwa muda mchache

kwa haraka sana au "bila kutazamia"

Proverbs 6:16

vitu sita ambavyo Yahwe huchukia, saba ambavyo

Maana yake: Yahwe huchukia vitu vingi na wala si mara moja.

ambavyo vinamchukiza

"amabavyo husababisha ajisikie karaha"

Proverbs 6:17

Sentensi Unganishi

Hii ni orodha ya vitu ambayo Yahwe huchukia kama vilivyotajwa katika 6:16

macho...ulimi... mikono... moyo...miguu

Sehemu zote hizi za mwili zinamwelezea mwandamu kamili "watu"

humwaga damu ya

"kuua" au "uuaji wa mtu kwa kusudi"

njama mbaya

"mipango miovu"

anong'onaye uongo

"kusema uongo siku zote"

mafarakano

agalia 6:14

mtu apandaye mafarakano

"mtu amabaye huondoa maelewano"

Proverbs 6:20

tii amri ya baba yako... usiyaache mafundisho ya mama yako

Maana yake baba na mama wote wanahusika katika kufundiha na mchakato wa kufunza

usiayache mafundisho ya mama yako

"tii mafundisho ya mama yako"

yafunge katika moyo wako; yakaze kwenye shingo yako

Hizi ni amri na maelekezo kama zimeandikwa unaweza kuziweka katika mwili wako au kuvaa mwilini mwako ili kujikumbusha mwenyewe.

Proverbs 6:22

Wakati unapotembea... unapolala... unapoamka

Hii inasisitiza kuwa masomo yanathamani muda wote

yatakuongoza... yatakulinda...yatakufundisha

mwandishi anarudia rudia kuonesha kuwa masomo haya yanathamani kwa vitu vya namna yoyote.

taa..mwanga...njia ya uzima

masomo yanafanya maisha kuwa mazuri na rahisi." yana faida kama taa...yanasidia kama mwanga katika giza..ni muhimu kuyafuta kama njia ya kuishi"

njia ya uzima

"njia inayoenda kwenye uzima" au "njia ya kuishi ambayo Mungu ameiruhusu"

Proverbs 6:24

itakutunza dhidi ya

"inakuokoa kutoka" au "inakulinda kutoka"

mwanamke mwovu...mwanamke mwovu

"malaya" pia angali 5:3

mwovu

"mbaya kimaadili"

uzuri wake

"kile kilicho kizuri kwake"

akunase

"kuwa na hali ya kudhibiti"

kope za macho yake

"macho yake mazuri"

Proverbs 6:26

bei ya kipande cha mkate

Hapa inaongelea gharama ya vitu siyo gharama ya kiroho au gharama ya maadili "kidogo"

atagharimu uhai wako

"mke wa mtu mwingine ataangamiza maisha yako kwa sababu kila wakati anahitaji zaidi" au "mume wa mke atakuwinda na atakuua"

Mtu anaweza kubeba moto kwenye kifua chake bila kuunguza nguo zake?

Jibu ni hapana "Kila mume ambaye hubeba moto kwenye kifua chake ataunguza nguo zake."

bila kuunguza

"bila kuteketeza" au "bila kuharibu"

nguo zake

nguo zinawakilisha mtu mwenyewe.

Proverbs 6:28

Mtu anaweza kutembea juu ya makaa ya moto bila kuungua miguu yake"

jibu ni hapana. "kila mtu anayetembea juu ya makaa ya moto miguu yake itaungua"

kutembea juu ya makaa ya moto

Hii inamaanisha kufanya uzinzi

kutembea

ni kwenda mwendo wa polepole kwa umbali mrefu ukitembea

kuungua

chomeka

Proverbs 6:30

kumdharau mwizi

" hawamtazami mwizi kwa dharau" au " hawafikiri mwizi ni mwovu"

kama atakamatwa

"mtu akimkamata"

katika nyumba yake

"ambayo anamiliki"

Proverbs 6:32

Mtu

"mwanaume"

ambacho anasitahili

'adhabu sitahiki kwa kile alichafanya"

aibu yake

" atakuwa na kumbukumbu za tendo lake la aibu"

Proverbs 6:34

hasira

"udhika sana"

hataonesha huruma

mtu ambaye mke wake amezini na mwanaume wingine " atakuumiza kadri anavyoweza"

wakati wa kulipiza kisasi

"kipindi analipza kisasi"

kulipiza kisasi

ni mtu kusababisha maumivu kwa mtu mwingine ambaye alitangulia kumwumiza hapo mwazo

fidia

"malipo"

hataweza kununuliwa

"hutaweza kumlipa pesa za kutosha kuibadili akili yake"

ingawa

"hata kama"

utampa

"kutoa kitu" au "kuadidi kutoa"

Proverbs 7

Proverbs 7:1

Tunza maneno yangu

"Tii maneno yangu"

uzihifadhi amri zangu ndani yako mwenyewe

"zikariri amri zangu"

tunza maagizo yangu

"tii maagizo yangu"

kama mboni ya jicho lako

Mboni ya jicho ipo ndani ya jicho ambayo watu huilinda sana wakati kitu kinaporukia usoni. "Mboni" inawakilisha kitu ambacho mtu hukithamini na kukilinda zaidi. "kama mali yako yenye thamani zaidi"

uzifunge katika vidole vyako

  1. mwandishi alitaka mwanae achore baadhi ya amri za Mungu kwenye pete na kuivaa au 2) mwandishi alitaka mwanae akumbuke daima amri za Mungu, kana kwamba ni petefulani ambayo aliivaa daima

ziandike kwenye kibao cha moyo wako

"zikumbuke vizuri amri zangu kana kwamba umeziandika kwenye jiwe"

Proverbs 7:4

Mwabie hekima, "Wewe ni dada yangu"

"Thamini hekima kama ambavyo ungempenda dada yako"

mwite ufahamu jamaa yako

"ufahamu uchukulie kama ambavyo ungemtendea jamaa yako"

jamaa

"ndugu" au "mmoja wa wanafamilia"

mwanamke malaya

Maana yake ni mwanamke yeyote ambaye mwanaume hajamwoa. " Mwanamke ambaye hupaswi kufanya naye chochote"

Mwanamke mwovu

Hii inamaanisha ni kwa mwanamke yoyote ambaye hajulikani kwa mwanaume

kwa maneno yake laini

"ambaye huongea vitu vya kufurahisha, lakini anataka kukudanyanya"

Proverbs 7:6

shubaka

ni wavu wa dirishani

Wajinga

"bila uzoefu, isiyo komavu/uchanga"

Proverbs 7:8

kona yake

"kona ambapo mwanamke mgeni alikuwa amesimama"

Kona

sehemu ambayo barabara mbili zinakutana

wakati wa jioni

muda ambapo giza linaanza kuingi na karibu kuwa giza

Proverbs 7:10

mwenye moyo wa uongo

Hapa "moyo" unamaanisha makusudi au mipango " mwanamke anakusudia kumdanganya mtu"

Alikuwa mwenye kelele na ukaidi

"aliongea kwa sauti sana na kutenda kwa namna aliyopenda"

miguu yake haikutulia nyumbani

"hakukaa nyumbani"

alisubiri kuvizia

"alisubiri kumnasa mtu"au "alisubiri ili ampate mtu ambaye ataweza kumshawishi kutenda dhambi"

Proverbs 7:13

yeye

Yeye inawakilisha mwanamke ambaye alitajwa katika 7:10

akamshika

"alimshikilia kwa nguvu"

kwa uso na haya

"kwa uso usiokuwa na hisia za aibu"

Mimi nimelipa nadhiri zangu

"nimetimiza dhabihu zangu nilizoahidi kwa Mungu"

kuutafuta uso wako

"kukutafuta" au "kukutafuta mahali ulipo"

Proverbs 7:16

nimekinyunyiza kitanda changu kwa

"nimetandaza juu ya kitanda changu"

udi

aina ya magamba kutoka kwenye mti ambayo hunukia vizuri

mdalasini

hiki ni kiungo kinachotengenezwa kutokana na magamba ya mti ambayo hunukia vizuri na radha nzuri

tushibe kwa upendo

"tufanye mambo ya upendo kwa kila mmoja kadri tunavyotaka"

Proverbs 7:19

hayupo nyumbani kwake

"hayupo nyumbani"

Mwezi mpevu

nyakati ambapo mwezi utoa mwanga sana

akamgeuza

"mwanamke akamshawishi mwanaume"

yeye...yake

mwanake aliyeolewa anayetaka kulala na mwanaume kijana

midomo laini

"kufurahisha kwa maneno ya kudanganya"

alimpotosha

"alimshawishi kufanya jambo baya" au alimshawishi kufanya dhambi pamoja naye"

Proverbs 7:22

ghafla akamfuata

"kwa haraka aliamua kwenda pamoja naye"

kama maksai akienda...kwenye mtego

ujinga na pasipo kutarajia kijana namfuata malaya ni kama vile wanyama ambavyo huwa hawajui hatari ambayo huwa inawakabili.

machinjo

sehemu ya kuulia mnyama ili kula nyama yake

ayala

angalia 5:18

Hadi mshale umtoboe hadi kwenye ini lake

"mpaka mwindaji ampige kwenye sehemu zake nyeti zaidi"

ini

kiungo hiki kinawakilisha sehemu muhimu sana ya mwili wa ayala

ingekuwa gharama ya uhai wake

" angeweza kufa haraka"

Proverbs 7:24

Sasa

Hii ni kuleta usikivu kwa wana wa msemaji anapohitimisha funzo hili

Moyo wako usizigeukie njia zake

"moyo wako ukae mbali kutoka kwenye njia za mwanamke malaya" au " Usiruhusu moyo wako ufanye mambo ambayo mwanamke malaya hufanya"

moyo wako

Hapa moyo unawakilisha matamanio ya mtu

usipotee katika njia zake

"usiiache njia sahihi ili kuzifuata njia zake"

Proverbs 7:26

amesababisha watu wengi kuanguka hali wamejeruhika

"amesababisha watu wengi kufa"

nyumba yake ipo kwenye njia za kwenda kuzimu ... hutelemka chini

Hapa "njia" inawakilisha aina ya tabia ambayo hufuatwa na watu wapumbavu. Kuzimu ilikuwa jina la ulimwengu wa wafu

kwenye njia za kwenda kuzimu...chini kwenye vyumba vyenye giza la mauti

maana yake wahanga wa mwanamke wataangamia

vyumba vyenye giza la mauti

Hapa inaonesha picha ambapo wafu wamelala katika vyumba mbalimbali huko kuzimu

Proverbs 8

Proverbs 8:1

Maelezo ya Jumla

Hekima ananena kwa watu katika mistari 4-36

Maelezo ya Jumla

Mistari mingi katika sura ya 8 ni mlinganisho au usambamba

Je Hekima haiti?

Hekima anaita

Je Hekima haiti?

Maana yake 1)Je hekima siyo kama mwanamke ambaye huita? 2) Je mwanamke aitwaye Hekima haiiti?

Je Ufahamu hapazi sauti yake?

Hapa neno "Ufahamu" ni sawa na neno "Hekima"

malango kwenye njia ya kuingia mjini

Nyakati za kale, miji mara nyingi ilikuwa na kuta za nje pamoja malango.

anaita

Hekima imevikwa sifa ya utu kama mwanamke(angalia Tashhisi)

Proverbs 8:4

Maelezo ya Jumla

Hekima ananena kwa watu katika mistari 4-36

sauti yangu ni kwa ajili ya wana wa wanadamu

Hapa "sauti" inawakilisha maneno yote yaliyoongewa "maneno yangu ni kwa ajili ya wana wa wanadamu"

wana wa wanadamu

"watu wote"

wajinga

"bila uzoefu, isiyo komavu/uchanga"

kujifunza hekima

"kujifunza namna watu wenye busara hutenda" au "kujifunza maana ya kuwa mwenye busara"

lazima mpate akili ya ufahamu

"lazima muanze kufahamu vitu kwa akili zenu"

Proverbs 8:6

wakati midomo yangu inapofunguka

Midomo inamaanisha kinywa cha mtu anayeongea " wakati nipofumbua mdomo wangu kuongea"

adili

"sawa" au "haki"

kinywa changu hunena

" mimi ninasema"

kilicho cha kweli

"kile ambacho watu wanapaswa kuamini"

uovu ni chukizo katika midomo yangu

"uovu ni chukizo kwangu" au "kusema vitu viovu ingekuwa ni chukizo kwangu"

uovu

inamaanisha maneno maovu

Proverbs 8:8

maneno ya kinywa changu

"mambo ninayofundisha"

lililogeuzwa

"uongo"

yamenyooka

"kweli na safi "

maneno yangu yapo wima kwa wenye kujipatia maarifa

"wale wanaojua maana ya haki na uovu hufahamu kuwa ninachafundisha ni sahihi"

wima

"kweli"

Proverbs 8:10

jipatie mafundisho yangu kuliko fedha

"fanya juhudi zaidi kufahamu mafundisho yangu kuliko kujipatia fedha"

Maana Hekima ni bora zaidi kuliko malijani; hakuna hazina inayolingana naye.

"Maana mimi Hekima ni bora kuliko malijani, hakuna hazina inayolingana na mimi"

Proverbs 8:12

Mimi, Hekima, huishi kwa Busara

Busara imeongelewa hapa kama mtu

Busara

"kuamua vema"

Mimi humiliki maarifa na busara

"Mimi ni mwenye maarifa na busara" au " Ninajua vitu vingi, na mimi ni mwangalifu"

busara

kuwa mwangalifu kuhusu kile unachosema na kufanya; kuwa na tahadhari usisababishe maumivu au uharibifu kwa wengine

kauli za udanganyifu

"maongezi mabaya"

udanganyifu

iliyogeuka kutoka kwenye haki

Proverbs 8:14

ushauri mzuri

mapendekezo ya busara

ushauri

mausia ambayo hutolew ili kumsaidia mtu

sahihi

nzuri, ya kutegemewa

Mimi ni utambuzi

"Mimi ni utambuzi"

wakuu

moja ya wanachama wa familia muhimu katika taifa

Proverbs 8:17

nawapenda

Huu ni upendo wa asili kati ya marafiki au ndugu

bidii

kuedelea kwa nguvu na uangalifu

Kwangu kuna utajiri na heshima

"Mimi ninautajiri na heshima"

utajiri unaodumu na haki

"kwa hiyo, nitatoa utajiri wa kudumu na haki kwa wale wanaonitafuta"

haki

"uwezo wa kuishi aktika njia iliyo safi"

Proverbs 8:19

Matunda yangu

ambacho hekima huzalisha au husababisha

faida yangu

manufaa au faida ambayo hekima husababisha

Natembea katika njia ya haki

"Ninaishi kwa haki" au " Ninatenda ambacho ni haki"

katikati ya njia za uadilifu

"Ninafanya mambo makalifu" au "Ninatenda ambacho ni haki"

hazina

ghala kwa ajili ya vitu vya thamani

Proverbs 8:22

kwanza katika matendo yake

"nilikuwa wa kwanza miongoni mwa vitu alivyoviumba"

nyakati za kale

"muda mrefu uliopita"

nyakati

muda mrefu

Niliumbwa

"Mungu aliniumba"

toka mwazo wa dunia

"tokea wakati ambapo Mungu aliiumba dunia"

Proverbs 8:24

Maelezo ya Jumla

Hekima anaendelea kuongea

Kabla milima kuwepo

"Kabla Mungu hajaifanya misingi ya milima na kuiweka mahali pake"

Proverbs 8:26

Nilizaliwa ...nilikuwepo

Hekima anaongea kuhusu yeye mwenyewe

nilizaliwa

"nilikuwa hai"

thibitisha

" umbwa" au "fanywa"

alipochora duara juu ya sura ya kina

"wakati alipoweka alama juu uso wa bahari umbali ambao mtu anaweza kuona katika bahari kwa kila upande"

kina

"bahari"

Proverbs 8:28

Maelezo ya Jumla

Hekima anaendela kunena

imarisha

kuweka katika maisha ya kudumu

wakati chemchemi katika kina zilipoimarishwa

"wakati Mungu alipoimarisha chemchemi katika kina"

chemchemi katika kina

Waebrani wa zamani waliamini bahari ilipata maji yake kutoka katika chemchemi kwenye kitako cha bahari

alipoumba mpaka kwa ajili ya bahari

"alipoumba ufukwe kwa ajili ya bahari"

pale alipoweka mpaka kwa ajili ya misingi ya nchi kavu

Neno la kiebrania "dunia" pia linamaanisha "nchi"

"pale alipoweka mpaka kwa ajili ya misingi ya nchi kavu"

"wakati Mungu alipoweka mpaka kwa ajili ya misingi ya dunia"

Proverbs 8:30

Nilikuwa ubavuni wake

Hekima anasema alikuwa karibu na Yahwe, kumaanisha kuwa alikuwa msaidizi wake katika kuumba dunia.

fundistadi mjuzi

Huyu ni mtu amabye aliyefundishwa kwa miaka kutengeneza vitu vizuri kwa matumizi kama samani au nyumba

furaha

chanzo cha raha au sababu ya kufurahi

siku kwa siku

"muda wote"

dunia yake yote

"ulimwengu wote alioumba" au " aliumba kila kitu"

wana wa wanadamu

"watu aliowaleta kuishi ulimwenguni"

Proverbs 8:32

Sasa

Hii ni kuleta usikivu kwa wana wa msemaji anapohitimisha funzo hili

Nisikilizeni

Hekima anaendelea kuongea juu yake mwenyewe

wale wanaozifuta njia zangu

"wale wanaofanya kile ninachofundisha"

usiziache

"hakikisha unazifuata"

ataangalia kila siku kwenye milango yangu, akisubiri pembeni ya nguzo za milango yangu

"mtu mwenye busara husubira nje ya nyumba ya hekima wakati wa asubuhi ili ampe huduma" au "mtu mwenye busara husubira nje ya nyumba ya hekima ili hekima aje na kumfundisha"

Proverbs 8:35

Anionaye mimi....Anionaye mimi... hunichukia

Hekima anaongea juu yake yeye mwenyewe

yeye anayeshindwa

" yeye anayekosa kuniona mimi"

maisha yake mwenyewe

"maisha"yanawakilisha mtu mwenyewe

Proverbs 9

Proverbs 9:1

Maelezo ya Jumla

Mistari hii inatoa mfano ambayo hekima inafikiriwa kuwa mwanamke anayetoa ushauri mzuri kwa watu.

Hekima ameijenga nyumba yake

Mwandishi anazungumza kuhusu hekima kana kwamba ni mwanamke ambaye ameijenga nyumba yake mwenyewe.

Amechinja wanyama wake

"amechinja wanyama kwa ajili ya nyama kwa chakula chajioni"

amechanganya mvinyo wake

katika Israeli ya kale watu walichanganya mvinyo kwa maji "ameandaa mvinyo wake kwa kuuchanganya kwa maji"

Ameandaa meza yake

"ametayarisha meza yake"

Proverbs 9:3

Maelezo ya Jumla

Mistari hii inaanza kutoa ujumbe wa Hekima, ambayo imepewa sifa ya mtu mwanamke.

amewatuma wafanya kazi wake

Hawa wafanyakazi walikwenda na kuwakaribisha watu kuja kwenye sherehe ambayo Hekima ametayarisha.

wafanya kazi wake

Vijana wa kike au wasichana ambao wapo kwenye huduma ya heshima, mwanamke mzima, kama vile Hekima.

anaita

" anatangaza" au " anawaalika". "kwa sauti kuu anarudia kuwakaribisha"

sehemu ya juu kabisa ya mji

Mwaliko unatangazwa kwenye sehemu ya juu kabisa ili watu wote wausikie vizuri

nani ambaye ni mjinga?...mtu alinayepungukiwa na akili njema

" mtu yeyote ambaye ni mjinga,...yeyote anayepungukiwa na akili njema"

ni mjinga

"bila uzoefu, isiyo komavu/uchanga"

ageukie hapa

" aiache njia yake na aje kwenye nyumba yangu"

Proverbs 9:5

Maelezo ya Jumla

Mistari hii inaendeleza ujumbe wa Hekima

njoo...kula...kunywa...ondoka ..ishi ...tembea

Mri hizi zote zipo kwenye wingi; Hekima anahutubia watu wengi kwa wakati mmoja.

mvinyo niliouchanganya

katika Israeli ya kale watu walichanganya mvinyo kwa maji "ameandaa mvinyo wake kwa kuuchanganya kwa maji"

acheni matendo ya ujinga

"acheni tabia yenu ya ujinga"

matendo ya ujinga

"bila uzoefu, isiye na ukomavu au mwenye hali ya uchanga"

njia ya ufahamu

"namna ya kuishi ambayo mtu mwenye busara huishi"

Proverbs 9:7

Maelezo ya Jumla

Mistari hii inaendeleza ujumbe wa Hekima

Mwenye kumwadibisha... wenye kumkemea

Tungo zote mbili zina maana sawa.

mwenye dhihaka

"mtu anayetukana watu wengine" au " mtu ambaye anapenda kuwafanya watu wengine waonekane wabaya"

hupokea matusi

"hupokea matendo ya kikatili"

mwenye kumkemea

"mtu yeyote anayemwelekeza"

usimkosoe

"usimwelekeze"

mkosoe mtu mwenye busara, na yeye...mfundishe mtu menye haki na yeye

'Kama utamwelimisha mtu mwenye busara, yeye...kama utamfundisha mtu mwenye haki , yeye"

mkosoe mtu mwenye busara...mfundishe mtu menye haki

Hivi virai viwili kimsingi vinasema jambo moja.

Proverbs 9:10

Maelezo ya Jumla

Mistari hii inahitimisha ujumbe wa Hekima

Hofu ya Yahwe

angalia katika 1:7

kwa njia yangu siku zako zitazidishwa

"Nitazidisha siku zako" au " Nitasababisha uishi siku nyingi"

kwa njia yangu

Hekima, imepewa utu kama wanamke, anaendelea kuongea hapa.

siku zako zitazisishwa, na utaongezewa miaka ya uzima

...hekima inafaida kubwa

utaongezewa miaka ya uzima

Nitaongeza miaka ya maisha yako" au "Nitaongeza miaka katika maisha yako" au "Nitakuwezesha kuishi muda mrefu"

Kama ni mwenye... na kama ni mwenye dharau

watu wenye busara hufaidika wenyewe kwa sababu ya hekima yao, na wenye dharau huteseka kwa sababu ya tabia zao.

utaichukua

Tabia mbaya wa mtu ni kama mzigo mzito ambao mtu huyo hupaswa kuubeba mgongoni mwake.

Proverbs 9:13

Maelezo ya Jumla

Mistari hii inaanza kuelezea upumbavu ambao umepewa sifa ya binadamu kama mwanamke

mwanamke mpumbavu

" upumbavu wa mwanamke"

hajafundishwa na hafahau kitu

Maana yake mwanamke mpumbavu asiyefaa " Hajui kitu chochote kabisa"

hajafundishwa

"Hajajifunza kutokana na auzoefu" au " Ni kijana na mjinga"

hutembea kwa unyofu katika njia yao

Hii ni nahau "Hufikira mambo yao mwenyewe tu" au " hujali shughuli zao wenyewe"

Proverbs 9:16

ni mjinga

"bila uzoefu, isiyo komavu/uchanga"

njoo hapa

'Acha njia yake na uje hapa"

humwabia

Huyu mwanamke mpumbavu ambaye ametambulishwa katika 9:13

wale ambao hawana akili

"ambao hawana hekima" au "wale wasio na busara"

Maji ya wizi ni matamu, na mkate wa siri hufurahisha sana

Mwanamke mpumbavu anaongea raha ya maji ya wizi na mkate unaoliwa kwa siri kuwaambia wanaume kuwa kama watalala naye watapata raha. Anasema "Unaweza kufurahia kwangu kama unavyofurahia maji ambayo umeyaiba au mkate ambao ni wa siri"

kwamba wafu wapo pale

"kwamba wanaume walikwenda kwake sasa wamefariki"

chini kuzimu

"kuzimu" humaanisha ulimwengu wa wafu.

Proverbs 10

Proverbs 10:1

Maelezo ya Jumla

Mistari mingi katika sura ya 10 niulingafu sambamba

mithali za Sulemani

Baada ya utangulizi katika Sura 1-9, Sura ya 10 inaanza mafundisho ya mithali; misemo mifupi inayofundisha hekima.

kusanywa

jipatia kitu kwa kipindi

Yahwe hataiacha nafsi ya mtu mwenye haki kwenda njaa

"Yahwe huhakikisha kwamba wale watendao haki wanapata chakula"

Proverbs 10:4

mkono mvivu

"Mkono" unawakilisha nguvu na uwezo wa mtu. KTN: "mtu asiyetaka kufanya kazi"

mkono wenye bidii

"Mkono" unawakilisha nguvu na uwezo wa mtu. "Mtu anayefanya kazi kwa nguvu"

Proverbs 10:6

juu ya kichwa

"kichwa" kinawakilisha mtu mwenyewe. " vimetolewa kwa"

kinywa cha waovu

"maneno wanayoongea waovu"

hufunika

hificha ukweli

jina

"kumbukumbu"

Proverbs 10:8

angamia

"kuharibiwa" au "kutofaa kwa matumizi"

udanganyifu

sio kweli, ongo, fedheha

Proverbs 10:10

yeye ambaye hukonyeza jicho

"ambaye hufanya alama kwa ashiria"

atashushwa chini

"wengine watamwangamiza"

kinywa cha mwenye haki

"maneno ya mtu mwenye haki"

ni maji ya chemchemi ya uzima

kauli ya mtu huyu mwenye haki ni kama chemchemi ya maji ilivyo kwenye nchi kavu, huhifadhi maisha ya wanyama na watu.

kinywa cha mwovu

"maneno ya mtu mwovu"

kinywa cha mwovu hufunuka vurugu

Mtu mwovu huonekana kusema mambo ambayo hayana madhara lakini mipango yake ni kuvuruga mambo dhidi ya wengine.

Proverbs 10:12

upendo hufunika

upendo hutenda kazi sawa na mtu huondoa shida kati ya watu badala ya kuichochea.

kwenye midomo ya mtu mwenye ufahamu

"ambayo mtu mwenye akili husema"

fimbo ni kwa ajili ya mgongo

"mtu asiye na akili anahitaji adhabu kali"

Proverbs 10:14

kinywa cha mpumbavu

"maneno ya mtu mpumbavu"

mji wake wenye ngome

"usalama wale"

Proverbs 10:16

mshahara..faida

Haya ni matokea ya kuteda mema au uovu

Kuna njia ya kwenda kwenye uzima kwa yule ambaye hufuata maonyo

"Mtu ambaye hutii mafundisho ya busara atakuwa mwenye furaha na maisha marefu"

lakini yule ambaye hukataa kurudiwa huelekea kupotea

"lakini yule ambaye hatii mafundisho ya busara hatakuwa na maisha mazuri"

Proverbs 10:18

ana midomo ya uongo

"husema uongo"

maovu hayakosi

"kuna dhambi nyingi"

Proverbs 10:20

ulimi wa mtu mwenye haki

"Chochote anachosema mtu mwenye haki"

fedha safi

fedha inawakilisha misemo ya thamani "... thamani mno"

hulisha

sababisha kuendelea au kuwa imara

Proverbs 10:22

Ubaya ni mchezo ambao mpumabavu hucheza

"Wapumbavu hufurahi katika ubaya"

Proverbs 10:24

kitamkuta kwa ghafla

shinda...

waovu ni kama dhoruba

kama ambavyo dhoruba huja na kuondoa kila kitu hivyo watu waovu hawataonekana

msingi unaodumu daima

"ni mwanzo kwa ajili ya jambo ambalo hudumu daima"

Proverbs 10:26

Kama siki kwenye meno na moshi kwenye macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale ambao wamemtuma

"siki" na "moshi" vinawakilisha mambo ambayo huumiza macho na meno ya mtu. " Kumtuma mtu mvivu kwenda kukamilisha kazi haifai na inaleta uchungu"

siki

kimiminika kichungu hutumiwa kwa radha au kutunza chakula.

miaka ya waovu

" muda wa kuishi mtu mwovu"

Proverbs 10:28

miaka ya waovu

"muda wa kuishi mtu mwovu"

hataondolewa

"atakuwa salama"

Proverbs 10:31

kwenye kinywa cha mtu mwenye haki

"Kwa maneno ya mtu mwenye haki"

ulimi wa udanganyifu utakatwa

"Mungu atafunga vinywa vya watu amabo husema uongo"

midomo ya mwenye haki huyajua yanayokubalika

"mtu mwenye haki hujua kuongoa kwa namna ya kukubalika"

kinywa cha waovu

"maneno ya waovu"

Proverbs 11

Proverbs 11:1

Maelezo ya Jumla

Mistari mingi katika sura ya 11 ni ulingafu sambamba.

Yahwe huchukia vipimo ambavyo si sahihi

"Mungu huchukia vipimo vya uongo" au " Mungu huchukia watu wanapodanganya"

lakini hufurahia katika kipimo sahihi

"lakini hufurahia njia za uadilifu" au lakini hufurahi watu wanapokuwa waadilifu"

Proverbs 11:3

waongo

"watu waongo" au "wale ambao ni waongo"

Utajiri ni ubatili kwenye siku ya ghadhabu

siku ya ghadhabu ni "siku ya hukumu" au "siku za mwisho". "utajiri wa mtu hatamsaidi wakati Mungu atakapokuja kuhukumu"

Proverbs 11:5

huinyosha njia yake

"anamwelekea safi"

waovu... waongo

" wale ambao ni waovu ... wale ambao ni waongo"

waongo hunaswa kwa ujanja wao

"Wale ambao hufanya ubaya hukamatwa kwa matamanio yao"

waongo

tayari kusaliti uaminifu; wasaliti, wadanganyifu

Proverbs 11:7

tumaini lilokuwa kwenye nguvu zake

"ujasiri aliokuwa nao kwa nguvu zake mwenyewe"

hupotea

"hutokomea"

Mtu mwenye haki hulindwa katika taabu

"Mungu humlida katika taabu mtu ambaye hutenda haki"

taabu huja

"taabu humpata"

Proverbs 11:9

Kwa kinywa chake mwovu

"maneno ya mwovu"

mji hukua

"makundi ya watu hufanikiwa" au "jumuiya hufanikiwa"

kwa kinywa cha wabaya

"maneno ya watu wabaya"

Proverbs 11:12

hulitunza jambo

"hujizuia kuongea juu ya jambo"

Proverbs 11:14

washauri

wale ambao hutoa mapendekezo ya kutendeka jambo; wanaoshauri

Proverbs 11:15

ambaye huchukia kutoa

"ambaye hukataa kutoa"

watu wasiokuwa na huruma

watu wakatili, bila huruma, korofi

hushika utajiri

"wanatamaa ya utajiri"

Proverbs 11:17

yule ambaye

"mtu ambaye"

hupanda ambacho ni haki

" hutawanya ambacho ni haki"

huvuna mshahara wa kweli

"hakika atapewa thawabu"

Proverbs 11:19

yule ambaye

"mtu ambaye"

hufuta mabaya

"hukimbilia uovu" au "hutafuta uovu"

ambao mioyo yao hufuata

"wenye mawazo maovu"

Proverbs 11:21

haikosi kupatiwa adhabu

"wataadhibiwa"

Kama pete ya dhahabu... bila ufahamu

mwanamke bila ufahamu hafai kama pete ya dhahabu kwenye pua ya nguruwe

bila ufahamu

"bila akili ya kawaida" au "ambaye ni mpumabavu"

Proverbs 11:23

yule ambaye hupanda mbegu

"mtu ambaye hujiandaa kwa wakati ujao"

nitakusanya hata zaidi

"nitajipatia hata zaidi"

asiyepanda

" asiye jiandaa"

Proverbs 11:25

atafanikiwa

"atapata zaidi"

yule ambaye

"mtu ambaye ni mkarimu" au" mtu yeyote"

mtu ambaye hukataa kuuza

mtu ambaye hubania utajiri wake badala ya kuwasaidia ambao ni wahitaji

yeye auzaye zawadi jema hukifunika kichwa chake

zawadi njema hutolewa kama taji ya heshima kwa yule ambaye huuza" au " mtu ambaye huiuza anaheshimiwa kwa baraka nyingi"

Proverbs 11:27

yule ambaye hutafuta kwa bidii

yule ambaye hutafuta kwa uangalifu na bidii

ataanguka

"ataangamizwa"

kama jani, watu wenye haki watasitawi

"watu wenye haki watafanikiwa kwa namna ile ile ambayo jani lenye afya hustawi"

watu wenye haki watasitawi

watu wenye haki watafanikiwa

Proverbs 11:29

ataurithi upepo

"hatarithi kitu chochote"

Proverbs 11:30

mwenye haki atakuwa kama mti wa uzima

"Wale watendao haki wataleta uzima kwao wenyewe na kwa wengine"

mti wa uzima

angalia 3:17

ni zaidi kiasi gani

"ni zaidi"

Proverbs 12

Proverbs 12:1

Maelezo ya Jumla

Mwandishi anatumia ulinganifu katika sura hii yote

Maelezo ya Jumla

katika mistari ya 1-15 analinganisha hekima na upumbavu

yeyoye

"mtu yeyote ambaye"

yule achukiaye sahihisho

"mtu ambaye hataki kuambiwa jambo la kufanya"

ni mpumbavu

"asiye na busara"

Proverbs 12:3

Mtu hawezi kuimarishwa kwa ubaya

"hakuna mtu anayeweza kuwa thabiti na salama kwa kufanya ubaya"

hataweza kung'olewa

"kung'olewa" kunawakilisha kuchomolewa kutoka ardhini kama mmea au mti. Hivyo hili haliwezi kutokea kwa watu watendao haki.

mke mwema ni taji ya mume wake

"mke mwema ni alama ya heshima kuu kwa mume wake"

yeye aletaye aibu ni kama ugonjwa ambao huozesha mifupa yake

"matendo ya aibu ya mwanake huharibu ushawishi wa mume wake na furaha"

Proverbs 12:5

maneno ya watu wabaya ni uviziaji kwa ajili ya kuua

"mabo ya udanganyifu ambayo watu waovu huyasema ni kama mtu anayevizia kuua mtu kwa kushitukiza"

maneno ya waadilifu huwahifadhi salama

"ushauri kutoka kwa mtu mwadilifu huwahifadhi watu salama"

waadilifu

wenye haki, waaminifu

Proverbs 12:7

watu waovu wametupwa

"Watu watawatupa watu waovu" au "watu watawaondoa watu wabaya kutoka kwenye mamlaka"

nyumba

"familia" au "uzao"

mtu husifiwa kwa namna ya wingi wa hekima yake

"watu watawasifu ambao wanahekima"

yule anayefanya uchaguzi wa udanganyifu huchukiwa

"watu watamchukia yule ambaye kila wakati huwaza mambo mabaya" au " watu watamchukia yule ambaye huchukua mambo mazuri na kuyabadilisha kuwa mabaya"

Proverbs 12:9

bora kupata cheo ambacho siyo muhimu

"Ni bora kuwa mtu wa kawaida"

ni mkatili

"husababisha mateso"

Proverbs 12:11

miradi

"mipango" au "shughuli"

matunda

matendo na wawazo hudhihirisha tabia ya mtu kama mti unavyodhilidhwa kwa matunda yake.

Proverbs 12:13

mtu mwovu hunaswa maongezi yake mabaya

"Mambo mabaya ambayo husemwa na mtu mwovu yatamnasa"

kama kazi ya mikono yake inavyompa thawabu

kama ilivyo kazi njema anayoifanya inampa thawabu"

Proverbs 12:15

macho pake mwenyewe

"katika maoni yake mwenyewe"

ushauri

mapendekezo ya busara

ni mwerevu

" ni mwenye busara" au "mwenye akili njema"

Proverbs 12:17

Maneno ya mtu ambaye hunena kwa haraka ni kama makali ya upanga

"anachonena mtu bila kufikiri kinaweza kuumiza sana kama kama vile amechoma kwa upanga"

ulimi wa mwenye busara

"amabyo watu wenye busara husema"

huleta uponyaji

"faraja na uponyaji"

Proverbs 12:19

midomo yenye uaminifu hudumu daima

"mtu mwaminifu udumu daima"

ulimi wenye kudanganya ni kwa kitambo tu

" yeye ambaye hudanganya hudumu kwa kitambo tu"

washauri

watu ambao hutoa mwongozo wa mapendekezo ili kufanyika jambo;

Proverbs 12:21

Hakuna mabaya yanayokuja

"mambo mema huja"

Yahwe anachukia midomo inayodanganya

"Yahwe huwachukia wale ambao husema uongo"

Proverbs 12:23

husitiri maarifa yake

"Huwa haongei kila kitu ambacho anakijua"

mkono wenye bidii

"watu wenye bidii"

afanyishwa kazi kwa nguvu

"atakuwa mtumwa"

Proverbs 12:25

Mashaka

hisia za woga au hofu, wasiwasi

zitamwelemea

"...tasababisha kuwa na huzuni au sikitishwa"

lakini neno zuri humfanya afurahi

" lakini wengine wapomsemesha kwa upole, hufurahia tena"

Proverbs 12:27

hawawezi kuoka mawindo yao wenyewe

"mawindo" maana yake ni wanyama waliokamatwa au kuuliwa wakati wa kuwinda. "kuoka" ni namna ya kupika chakula

utajiri wa thamani

"hazina yenye thamani"

Proverbs 13

Proverbs 13:1

Mwana mwenye busara husikia

"Mwana mwenye busara hutii"

hatasikiliza karipio

"hatajifunza kutokana na kukaripiwa" au "hataweza kutii japo atakaripiwa"

kutoka kwenye matunda ya kinywa chake

"kutoka kwenye maneno ya kinywa chake " au "kutokana na usemi wake"

hamu

shauku au kupendelea kitu

waongo

wale ambao wapo tayari kusaliti au kuwadanganya wengine

Proverbs 13:3

kinywa chake

" Ambacho ananena"

apanuaye midomo yake

"kuongea sana" au "kuzungumza mno"

hamu...hamu

Angalia 13:1

tamani sana lakini hapati kitu

"hamu ya kubwa sana lakini hapati kitu"

hamu ya watu wenye bidii itamalika kabisa

|"watu wenye bidii watapata maisha ya kutoshelezwa" au "kuwa na bidii kutawafanya watu watosheke kabisa"

watu wenye bidii

watu ambao hufanya kazi kwa uangalifu na nguvu endelevu

Proverbs 13:5

chukizo

sababisha hisia kali za kuchukia

haki huwalinda wale

"Njia ya kuishi iliyothibitishwa na Yahwe hulinda"

ambao hawana kasoro katika njia yao

"amabo hawana makosa katika njia yao ya kuishi" au "ambao huishi maisha ya uadilifu"

ubaya huwageuzia mabali wale ambao hutenda dhambi

"ubaya huwageza wenye dhambi kutoka katika njia ya mafanikio"

Proverbs 13:7

amabye hujitarisha mwenyewe

"ambaye hujifanyia utajiri yeye mwenyewe"

hasikii kitisho

  1. hakuna mtu atakaye mtisha kumwibia maana hana kitu cha kuibiwa au 2) hatasikiliza sahihisho la watu kwa sababu hana kitu cha kupoteza kama watamwadhibu " hasikilizi karipio"

Proverbs 13:9

Nuru ya watu wenye haki hufurahia

"ushawishi wa watu wenye haki huleta furaha"

taa ya watu waovu itazimishwa

"watu waovu watapoteza ushawishi wao"

Majivuno huzaa ugomvi

" Mara nyingi majivuno husababisha ugomvi"

sikiliza

"fuata" au "jali"

ushauri mzuri

maoni ambayo husaidia na kufaidisha

Proverbs 13:11

utajiri hudhoofika

"utajiri hupungua" au "utajiri hupotea taratibu "

kufanya kazi kwa mkono wake

"kufanya kazi kwa nguvu za mwili"

hufanya fedha yake istawi

"hufanya pesa yake iongezeke"

wakati tumaini linapositishwa

"wakati mtu anapotumaini kwa ajili ya jambo lakini hapokei hadi muda mrefu"

huvunja moyo

"husababisha huzuni kali"

shauku ikitimizwa ni mti wa uzima

mtu akipokea ambacho alitumaini na kufurahi ni kama mti unaotoa uzima. "shauku iliyotimizwa ni kama mti wa uzima"

mti wa uzima

"mti ambao unatoa uzima" au "mti ambao mtunda yake hutoa idhini ya uzima"

Proverbs 13:13

mwenye kuheshimu amri atapata thawabu

"watampa tuzo yeye ambaye anaheshimu amri"

chemchemi ya uzima

"chanzo kizuri cha uzima"

tanzi ya mauti

"mitego ambayo huekea kwenye mauti"

Proverbs 13:15

lakini njia ya mwongo haina mwisho

"lakini tabia ya waongo itasababisha uharibifu wao wenyewe"

mwongo

"mtu mwongo"

mpumbavu huonesha upumbavu wake

"mpumbavu huonesha upumavu wake kwa kila"

Proverbs 13:17

huanguka kwenye taabu

"hufanya kitu kibaya"

mjumbe

"tarishi" au "mtu wa mahusiano"

hujifunza katika sahihisho

"hujifunza ambapo mtu humsahihisha"

Proverbs 13:19

ni tamu

"yenye kuleta furaha" au "inafurahisha"

hamu

shauku au kupendelea kitu

ataumia

"ataangamia"

Proverbs 13:21

msiba huwakimbilia watenda dhambi

"mwenye dhambi hupata taabu popote wanapokwenda"

watu wenye haki hupewa thawabu ya mema

"Mungu huwapa thawabu watu wenye haki kwa mema"

wajukuu wake

"wana wa wana wake"au "watoto wa watoto wake" au "wazao wake"

utajiri wa mwenye dhambi umehifadhiwa kwa ajili ya mtu mwenye haki

" yeye atendaye haki atapokea utajiri ambao umahifadhiwa na mwenye dhambi"

Proverbs 13:23

shamba lisilolimwa

"shamba ambalo halijaandaliwa kwa kuzalisha chakula" au " shamba ambalo ni tupu tayari kwa kupanda"

lakini huondolwa kwa udhalimu

"lakini udhalimu hukichukua chakula" au " watu wadhalimu hukichukua chakula"

huzingatia kumwelekeza

" nakikisha namwelekeza"

Proverbs 13:25

hutimiza hamu yake

"hujiridhisha mwenyewe"au " hutimiza hamu yake"

tumbo la mwovu huona njaa daima

"mtu mwovu huwa na njaa daima kwa ajili ya kupata zaidi"

Proverbs 14

Proverbs 14:1

huijenga nyumba yake

"huifanya nyumba yake kuwa bora"

numba

  1. nyumba halisi, ambalo ni jengo anamoishi 2) inaweza kumaanisha familia yake

kwa mikono yake

"mikono" inawakilisha matendo anayofanya. "yeye mwenyewe" au "kwa namna ambavyo anajiheshimu"

yeye ambaye ... yeye ambaye

"mtu ambaye ... mtu ambaye"

huenenda kwa uadilifu

"huenenda katika njia ya haki na uaminifu katika maisha yake"

humdharau

"kukosa adabu" au " kuonesha kuchukia"

katika njia zake humdharau yeye

"zake" huyu ni mtu asiye mwamnifu na "yeye" ni kiwakilishi kumwakilisha Yahwe

Proverbs 14:3

kinywa cha ... midomo ya

Kinywa na midomo vyote vinahusiana na kile ambacho mtu hunena

kipukizi la kiburi chake

chipukizi ni kitu amabacho huota kutoka kwenye kitu kingine. " ambacho huzalishwa na kiburi chake"

busara

"watu wenye busara"

ataihifadhi

"atawalinda kutoka ktatika madhara" au " atawatunza salama"

hori la kulia

hori ni kontana ambapo huwekwa chakula kwa ajili ya wanyama

mazao mengi

"mavuno mazuri"

kwa nguvu ya maksai

"nguvu" inawakilisha kazi imara anayoweza kufanya maksai "kwa sababu ya kazi anayofanya maksai"

Proverbs 14:5

hupumua uongo

"hudanganya daima"

na hakuna kitu

"na hekima haipo pale" au "lakini hatapata hekima"

huja upesi kwa

"hupatikan kwa urahisi" au "hupata bila ugumu"

mtu mwenye ufahamu

"mtu mwenye hekima" au "mtu mwenye ufahamu"

Proverbs 14:7

kwenye midomo yake

"kwa kauli zake" au "kwa ushauri wake"

busara

mtu mwenye maamuzi mazuri au akili

njia yake mwenyewe

"mwenendo wake" au "namna ya maisha yake"

upumavu wa wapumbavu ni udanganyifu

upumbavu wa wapumbavu ni kufikiri kuwa wanabusara, wakati hawana.

Proverbs 14:9

wakati dhabihu ya hatia inapotolewa

...wapumbavu hawaombi msamaha kwa Mungu au watu kwa ajili ya mambo mabaya wanayofanya.

lakini miongoni waadilifu hushiriki fadhila

"lakini waadilifu hufurahia wema pamoja" au "Wema wa Mungu huonekana miongoni mwa waadilifu"

uchungu

"huzuni" au "simanzi"

hakuna mgeni

"wale wasiomfahamu"

Proverbs 14:11

hema

"kaya"

sitawi

"kufanikiwa sana"

kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu

"watu hufikiri kwamba namna wanavyoishi ni njia sahihi"

Proverbs 14:13

moyo huweza kucheka

"Hisia za mtu zinaweza zinaweza kuonesha furaha"

kuwa katika maumivu

"kukabiliwa na maumivu" au "umia"

yeye ambaye

mtu ambaye

stahiki ya njia zake

"anachostahili, hulingana na namna anavyoishi"

alivyo

" ambacho anakimiliki" au " ambacho anahaki ya kukifanya"

Proverbs 14:15

mjinga

"bila uzoefu, asiye mkomavu, bado na hali ya uchanga"

hatua zake

"matendo yake"

hugeukia mbali na uovu

"huepuka matendo maovu"

huacha kwa ujasiri

"hupuuza kabisa"

Proverbs 14:17

ni mwepesi kukasirika

"kuwa na hasira kwa haraka"

mjinga

"bila uzoefu, asiye mkomavu, bado na hali ya uchanga"

hurithi upumabavu

"rithi" maana yake kumiliki kitu kwa kudumu

upumabavu

mawazo na matendo ya kipumbavu

watu wenye busara

"watu werevu"

huvikwa taji ya maarifa

"vaa maarifa kama vile kilemba"

Proverbs 14:19

huinama chini

kuinama kwa unyenyekevu kuonesha adabu na heshima kwa mtu

kwenye malango ya mwenye haki

"kuonana na mtu mwenye haki"

mtu maskini huchukiwa hata na rafiki zake mwenyewe

"kila mmoja humchukia mtu maskini hata jirani zake"

Proverbs 14:21

yule...yule

"mtu ..mtu"

maskini

"watu fukara"

Je wale ambao hupanga mabaya hawapotei?

"wale ambao hupanga mabaya watapotea"

ambao hupanga mabaya

"amabo hufanya mipango ya uovu" au " amabo hufanya mipango ya mambo mabaya"

Proverbs 14:23

lakini kukiwa na maongezi tu

"lakini kama utaongea tu" au "lakini watu wote hufanya maongezi"

taji ya watu wenye busara

"thawabu ya watu wenye busara"

upumbavu wa wapumbavu

Angalia 14:7

Proverbs 14:25

hupumua uongo

"hudanganya daima"

Proverbs 14:26

chemchemi ya uzima

"chanzo cha maisha"

kutoka kwenye tanzi za mauti

"kutoka kwenye mitego ambayo italeta kifo"

Proverbs 14:28

idadi kubwa ya watu wake

"idadi ya watu anaowatawala"

ni uharibifu wa mfalme

"mfalme hana kitu na ufalme wake utaanguka"

mwepesi wa hasira

"mtu ambaye hukasirka haraka"

Proverbs 14:30

moyo mtulivu

" mtazamo wa amani" au "mwenendo ambao ni wa amani"

huozesha mifupa

"husababisha mtu kukosa afya mwilini na rohoni"

yule ambaye... yule ambaye

"mtu ambaye ... mtu ambaye"

laana

maana yake kutamani mambo mabaya yaweze kutokea kwa mtu.

maskini ...mhitaji

"mtu maskini...mtu mhitaji"

huonesha fadhila kwa

"ni mkarimu kwa" au " husaidia"

Proverbs 14:32

hushushwa chini kwa matendo yake mabaya

"matendo mabaya humsukuma" au " matendo mabaya huharibu"

Hekima hukaa katika moyo

"hekima ipo katika namna ya kufikiri na kutenda"

ufahamu

"mtu mwenye ufahamu"

hujidhihirisha yeye mwenyewe

" huhakikisha kuwa watu wanamjua"

yeye

neno "yeye" linawakilisha hekima

Proverbs 14:34

aibu

"kuleta fedheha "

kwa busara

"kwa werevu"

yule ambaye

"mtumishi ambaye"

Proverbs 15

Proverbs 15:1

jibu la upole huodoa ghadhabu

"kumjibu mtu kwa upole kutatuliza ghadhabu ya huyo mtu"

lakini neno la ukatili huchochea hasira

"lakini kuongea kwa ukali husababisha yule mtu kuwa na hasira zaidi"

ulimi wa watu wenye busara hutamka maarifa

"watu werevu hutamka maarifa wanapoongea"

hutamka maarifa

"huyafanya maarifa yavutie" au " hutumia maarifa kwa usahihi"

kinywa cha wapumbavu humwaga upumbavu

"wapumbavu huongea upumbavu siku zote"

Proverbs 15:3

macho ya Yahwe yapo kila mahali

"Yahwe huona kila kitu"

mema na maovu

"watu wema na watu waovu"

ulimi uponyao ni mti wa uzima

" maneno ya upole ni kama mti ambao hutoa uzima"

ulimi wenye kudanganya huvunja moyo

"kauli ya uongo husababisha mtu kuvunjika moyo"

Proverbs 15:5

yeye ambaye hujifunza kutokana na sahihisho

"yeye ambaye hujifunza wakati wa kusahihishwa na mtu mwingine"

busara

"werevu"

mapato ya mtu mwovu humpa

"utajiri ambao mtu mwovu hujipatia humpa"

Proverbs 15:7

midomo ya watu wenye busara husambaza maarifa

"kauli ya watu wenye busara hutawanya maarifa"

siyo mioyo ya wapumbavu

" wapumbavu hawasambazi maarifa" au " wapumbavu hawana maarifa katika mioyo yao" au "wapumbavu hawafahamu maarifa"

watu waadilifu

"watu wanaoishi kwa haki"

ni furaha yake

"humfurahisha"

Proverbs 15:9

Yahwe huchukia njia ya watu waovu

"Yahwe huchukia namna ambavyo watu waovu huishi"

yule ambaye huandama haki

"mtu ambaye hujitahidi kuishi kwa haki"

yeyote ambaye huiacha njia

"yeyote ambaye huacha kuishi kwa haki"

yeye ambaye huchukia sahihisho

"mtu ambaye huchukia wakati watu wengine wanapomwelekeza"

Proverbs 15:11

kuzimu na uharibifu vipo wazi mbele ya Yahwe

"Yahwe anajua kila kitu kuhusu sehemu walipo wafu"

Je ni zaidi mara ngapi kwa mioyo ya wana wa wanadamu?

hii ni nahau kumaanisha "mawazo ya wanadamu"

mioyo ya wana wa wanadamu

"mawazo ya wanadamu"

mwenye dharau huchukia sahihisho

"mwenye dharau huchukia wakati wa kurudiwa"

hatakwenda kwa wenye busara

"hatakwenda kwa wenye busara kutafuta ushauri wao"

Proverbs 15:13

moyo wenye furaha huufanya uso kuwa mchangamfu

"mtu anapokuwa na furaha, uso wake ni mchangamfu"

huvunja moyo

" humfanya mtu akate tamaa"

moyo wa mwenye ufahamu

"mtu mwenye ufahamu"

kinywa cha wapumbavu hula upumbavu

"watu wapumbavu hutamani upumbavu kana kwamba ni chakula ambacho wangekula"

Proverbs 15:15

siku zote za watu walidhulumiwa ni taabu

"watu waliokandamizwa wanataabu katika siku zao zote"

moyo mchangamfu unasikukuu bila kikomo

"mtu mchangamfu hufurahia maisha, kana kwamba anasherehekea sherehe isiyokuwa na mwisho"

unasikukuu bila kikomo

"sikukuu za daima"

mafadhaiko

"wasiwasi"

Proverbs 15:17

mlo wenye mboga

"mlo kidogo" au "chakula kidogo"

ambapo kuna upendo

" ambapo watu wanapendana kila mmoja"

huduma ya ndama aliyenona pamoja na chuki

"kutengewa ndama aliyenona kwa chuki"

ndama aliyenona

"mlo wa gharama' au "sherehe"

kwa chuki

"ambapo watu huchukiana"

huchochea mabishano

"husababisha watu kubishana zaidi"

Proverbs 15:19

njia ya mvivu ...njia ya mwadilifu

"maisha ya mvivu...maisha ya mwadilifu"

njia ya mvivu ni kama sehemu yenye uwa wa miiba

"maisha ya mvivu ni kama mtu anayejaribu kutembea kwenye uwa wa miiba"

njia ya mwadili ni njia panda iyojengwa

watu wenye uadilifu hupata baraka katika maisha yao kana kwamba wanatembea juu ya barabara nzuri

njia panda iyojengwa

Hii ni njia pana, tambarare na isiyo na vikwazo

Proverbs 15:21

mtu mwenye ufahamu hutembea katika njia iliyonyooka

"mtu mwenye ufahamu hutenda yaliyo sawa"

mipango hubatilika

"mipango hushindikana"

ambapo hapana ushauri

"wakati hakuna mtu wa kutoa ushauri"

washauri

watu ambao hutoa mwongozo wa mapendekezo kwa ajili ya shughuli

hufanikiwa

"mipango hufanikiwa"

Proverbs 15:23

jibu la kufaa

"jibu la kutosheleza" au " jibu linalofaa"

jinsi gani ni zuri neno kwa wakati wake

"neno ambalo mtu huongea kwa wakati sahihi ni zuri"

njia ya uzima huelekea juu....kutoka chini kuzimu

Mwandishi anaongelea namna ya kuishi ambayo matokeo yake ni uzima kama njia iendayo juu na namna ya kuishi ambayo matokea yake ni kifo ni kama njia iendayo chini kwenye sehemu ya wafu.

Proverbs 15:25

urithi

"nyumba" maana yake ni kaya, mali au utajiri.

maneno yenye upole ni safi

"maneno ya upole ni safi" au "maneno mazuri ni safi"

Proverbs 15:27

moyo wa mwenye haki hutafakari kabla ya kujibu

"mtu atendaye mema hutafakari cha kusema kabla ya kujibu"

kinywa cha watu waovu humimina mabaya yake yote

"watu waovu wanasema mambo mabaya daima"

kinywa cha watu waovu humimina mabaya yake yote

"moyo wa mtu mwovu humimina mabaya yake yote" au " vinywa vya watu waovu humwaga maovu yake yote"

Proverbs 15:29

Yahwe yupo mbali kutoka kwa watu waovu

"Yahwe awasikilizi watu waovu" au " Yahwe hawajibu watu waovu"

nuru ya macho

"kuonesha hisia za uchangamfu"

huleta furaha kwenye moyo

"mtu mwenye hisia za kuchangamka kwa sababu ya furaha" au "watu hupata furaha wanapomwona mtu mwenye hisia za uchangamfu"

habari njema ni afya kwenye mwili

"kupokea habari njema husababisha mtu ajisikie vizuri"

Proverbs 15:31

utabaki miongoni mwa watu wenye busara

  1. watu wataendelea kukufikiria kuwa mtu mwenye busara au 2) utaendelea kufurahia ushirika wa watu wenye busara.

Proverbs 15:33

hofu ya Yahwe hufundisha hekima

"mtu anapokuwa na hofu ya Yahwe, hujifunza kuwa na busara"

hofu ya Yahwe

angalia 1:7

unyenyekevu huja kabla ya heshima

mtu lazima kwanza ajifunze unyenyekevu kabla Yahwe hajamheshimu.

Proverbs 16

Proverbs 16:1

Mipango ya moyo huwa ni ya mtu

"mtu hufanya mipango katika akili zake"

kwa Yahwe huja jibu kutoka katika ulimi wake

  1. Yahwe hunena jibu lake katika mipango ya mtu -maana yake Yahwe hutambua matokeo ya mipango ya mtu au 2) Yahwe huwezesha mtu kunena juu ya mipango aliyoiandaa.

jibu kutoka katika ulimi wake

"jibu ambalo hunena"

Njia zote za mtu ni safi machono pake mwenyewe

mtu hudhani kwamba kila kitu anachofanya ni safi"

Yahwe huipima mioyo

"Yahwe hufanya uamuzi kwenye mawazo ya mtu"

Proverbs 16:3

hata waovu kwa ajili ya siku ya taabu

" hata waovu aliwaumba kwa ajili ya siku ya taabu"

Proverbs 16:5

kila mmoja mwenye moyo wa kiburi

"kila mtu mwenye kiburi"

hawatakosa kuadhibiwa

"Yahwe atawaadhibu"

kwa agano la uaminifu na mdhamana kosa hulipiwa

"Yahwe hulipa kwa ajili ya uovu kwa agano la uaminifu na mdhamana"

watu hugeuka kutoka katika uovu

"watu huacha kufanya mambo maovu"

Proverbs 16:7

huwafanya

"Yahwe hufanya"

pato kubwa

"kujipatia pesa nyingi"

udhalimu

tendo lisilo la haki

Proverbs 16:9

kwenye moyo wake mtu hupanga njia yake

"mtu hupanga katika akili jambo atakalofanya"

Yahwe huziongoza hatua zake

Yahwe huamua matokeo ya mipango ya mtu

ushauri upo kwenye midomo ya mfalme

"kila anachosema mfalme ni ushauri"

ushauri

uamuzi kutoka kwa Mungu, hukumu takatifu

katika hukumu kinywa chake hakisemi uongo

"anapotamka hukumu, huwa hasemi uongo"

kinywa chake hakisemi uongo

"husema kweli"

Proverbs 16:11

Vipimo vya kweli hutoka kwa Yahwe

Yahwe anataka haki na fadhila wakati wa kufanya biashara. Watu ambao si waadilifu hutumia vipimo vizito au vyepesi katika vipimo vyao ili kupata zaidi wanaponunua au kuuza.

vipimo vyote katika begi ni vya kwake

  1. Yahwe tayari amebainisha namna kila kipimo kitakavyo pima 2) Yahwe anahusika kwa kila kipimo abacho mfanyabiashara hutumia.

hicho ni kitu cha kudharauliwa

"hicho ni kitu ambacho watu hukidharau" au "hilo ni jambo ambalo Yahwe hulichukia"

maana kiti cha enzi huthibitishwa kwa kutenda haki

"maana mfalme huthibitisha utawala wake kwa kutenda haki"

Proverbs 16:13

midomo ambayo husema haki

"mtu ambaye husema kweli"

ghadhabu ya mfalme ni mjumbe wa kifo

"mfalme mwenye hasira anaweza kuua watu"

Proverbs 16:15

Maelezo ya Jumla

mstari wa 15 unapinga na ule wa 14

katika nuru ya uso wa mfalme kuna uzima

"mfalme anapofurahi, watu huishi"

fadhila zake ni kama wingu ambalo huleta mvua ya masika

mfalme anapoonyesha fadhila kwa mtu ni kama wingu ambalo huleta mvua kukuza mazao

Ni bora kiasi gani kujipatia hekima badala ya dhahabu

"Ni bora sana kupata hekima kuliko kupata dhahabu"

yapasa zaidi kuchagua kupata ufahamu kuliko fedha

"Mtu anapaswa kuchagua kupata ufahamu zaidi kuliko kupata fedha"

Proverbs 16:17

Njia kuu ya watu waadilifu

"njia ya haki ambayo watu waadilifu huishi "

kuacha uovu

"kuwalinda kutoka katika kutenda mabaya"

moyo wa kiburi

"tabia ya majivuno"

anguko

"maangamizi" au " kushindwa"

Proverbs 16:19

nyara

vitu vilivyochukuliwa katika mapigano

walichofundishwa

"walichojifunza"

Proverbs 16:21

yule mwenye busara katika moyo wake anaitwa ufahamu

" watu watamwita ufahamu yule mwenye busara katika moyo" au " yule mwenye busara katika moyo atapata heshima ya kuwa mtu mwenye ufahamu"

utamu wa kauli

"kauli ya upole" au "kaui ya kufurahisha"

ufahamu ni chemchemi ya uzima

" ufahamu ni kama chemchemi itiririkayo maji yanayotoa uzima"

Proverbs 16:23

moyo wa mtu mwenye busara hutoa

"mawazo ya mtu mwenye busara hutoa"

hutoa utambuzi kwenye kinywa chake

"hufanya kauli yake kuwa ya busara"

kwenye midomo yake

"yale anayosema"

maneno yakupendeza ni sega la asali

"maneno ya kupendeza ni kama sega la asali"

matamu kwenye nafsi

  1. inawakilisha hamu na shauku ndani ya mtu "tamu kiasi kiasi cha kutosha kumfanya mtu afurahi" au 2) "tamu kwa radha"

uponyaji kwenye mifupa

"uponyaji katika mwili"

Proverbs 16:25

kuna njia ambayo huonekana swa kwa mtu

"mtu hufikiria kwamba namna anavyoishi ni sawa"

lakini mwisho wake ni njia kuelekea kwenye mauti

ni njia kuelekea kwenye kifo

shauku ya mfanyakazi hufanyakazia kwa ajili yake

"mfanyakazi hushughulika kutimiza hamu yake"

njaa yake humhimiza

"huendelea kufanyakazi kwa sababu ya njaa yake"

Proverbs 16:27

mtu asiyefaa huchimba madhara

"mtu asiyefaa hutafuta madhara kana kwamba anachimba kitu chini ya ardhi"

asiyefaa

"mwovu"

madhara

"ubaya" au "taabu"

kauli yake ni kama moto unaounguza

"huumiza watu kwa maneno yake, kama moto unaounguza vitu"

mmbeya

mtu ambaye husema uzushi au husambaza uvumi

Proverbs 16:29

mtu mwenye jeuri hulala kwa jirani yake

"mtu mwenye jeuri humshawishi jirani yake"

mtu mwenye jeuri

"mtu jeuri" au "mtu ambaye hutenda vurugu"

humwogoza katika njia isiyo nzuri

"humsababisha kufanya mambo yasiyo mazuri"

njia isiyo nzuri

"njia mbaya sana"

yule ambaye hukonyeza jicho lake...wale ambao hudhibiti midomo

angalia 10:10

wataleta maovu

"atafanya mambo mabaya"

Proverbs 16:31

mvi ni taji ya utukufu

"mtu aliyeishi muda mrefu wa kutosha kupta mvi ni kama yule anayevaa taji kichwani pake"

ni faida

"mtu hupata faida"

anayetawala roho yake

"yule anayetawala hasira yake"

Proverbs 16:33

kura hurushwa kwenye mikunjo

"mtu hurusha kura kwenye mkunjo wake"

uamuzi hutoka kwa Yahwe

Yahwe huamua namna kuanguka kura au si kura lakini Yahwe ambaye huamua nini kitokee.

Proverbs 17

Proverbs 17:1

kuwa na utulivu

Hapa "utulivu" unawakilisha "amani" "kuwa na amani"

kuliko nyumba iliyojaa sherehe pamoja na ugomvi

"kuliko kuwa katika nyumba iliyojaa sherehe ambayo inaugomvi"

Proverbs 17:3

Kalibuni kwa ajili ya fedha na tanuru kwa ajili ya dhahabu

"karibuni hutumika kusafisha fedha na tanuru hutumika kusafisha dhahabu"

Yahwe husafisha mioyo

Yahwe huwajaribu watu ili kuwasaidia kuacha ubaya na upumbavu...hivyo Yahwe husafisha kuondoa kila kitu ambacho si safi. "Yahwe huijaribu mioyo ya watu"

mioyo

...mawazo na hamu za watu

midomo miovu

"mtu mwovu" au "maongezi mabaya"

hutega sikio

"husikiliza"

ulimi wa uharibifu

"mtu mharibifu" au "maongezi ya uharibifu"

Proverbs 17:5

maskini

"wale ambao ni maskini"

Muumba wake

" yule ambaye alimuumba"

kwa bahati mbaya

"kwa taabu za watu wengine"

ni taji ya

"huleta heshima na taadhima kwa"

wazee

" wale ambao ni vikongwe" au "watu wenye umri mkubwa"

Proverbs 17:7

kauli ya kushawishi

"kauli nzuri"au "kauli nzuri"

midomo ya uongo haifai kabisa kwa mkuu

"Haifai kabisa kwa mkuu kudanganya"

hongo ni kama jiwe la miujiza kwa yule atoaye

"hongo hufanyakazi kama jiwe la miujiza kwa yule anayeitoa" au "hongo hufanya kazi kama jiwe la miujiza kwa yule anayetoa rushwa"

kila anapogeuka

" kwa kila anachofanya" au "kila anachojaribu kufanya kwa kutoa hongo"

Proverbs 17:9

kosa

jambo ambalo huumiza au humkasirisha mtu

ambaye hurudia jambo

"ambaye hurudia kosa la nyuma"

huondoa

"hutenganisha"

karipio huenda ndani ya mtu ...kuliko mapigo yaendayo ndani ya mpumbavu

"karipio utendaji mwingi kwa mtu... kuliko mapigo mia kwa mpumbavu"

mtu mwenye ufahamu

"mtu anayefahamu"

mapigo mia kwenda

"mamia ya mapigo kwenda"

Proverbs 17:11

hutafuta uasi

hutafuta kuasi

mjumbe katili atatumwa dhidi yake

"mjume katili atakuja dhidi yake"

atatumwa dhidi yake

"atatumwa kwenda kumdhuru"

dubu aliyeibiwa watoto wake

"dubu ambaye aliyepoteza watoto wake"

katika upumbavu wake

"ambaye hufanya upumbavu"

Proverbs 17:13

ubaya hautaondoka katika nyumba yake

"mambo mabaya hayatakoma kutokea kwake na familia yake"

mwanzo wa faraka ni kama mtu ambaye humwaga maji kila mahali

"kuanzisha ugomvi ni kama kusukuma maji na na kuruhusu yaende kila mahali"

kupasuka

"kuanza"

Proverbs 17:15

Yule ambaye humwacha huru mtu mwovu na mtu ambaye humlaumu mtu mwenye haki

" Yule ambaye huwaacha huru watu waovu na yule ambaye huwalaumu mwenye haki"

humwacha huru

halalisha, tangaza mtu kuwa hana hatia

kwa nini mpumbavu yapasa alipe pesa kujifunza juu ya hekima, wakati hana uwezo wa kujifunza juu yake?

"mpumbavu hapaswi kulipa pesa kujifunza juu ya hekima kwa sababu hana uwezo kujifunza juu yake"

Proverbs 17:17

ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa taabu

"ndugu yupo kwa ajili ya wakati wa taabu"

akili

"maamuzi ambayo si mazuri"

ahadi za lazima

ahadi ambazo ni lazima zitimizwe na mara nyingi ni mzigo kwa yule anayefanya ahadi hii

Proverbs 17:19

husababisha mifupa kuvunjika

"husababisha mtu kusafiri na kujiumiza mwenyewe"

mwenye moyo mdanganyifu

"ambaye ni mdanganyifu" au "asiye mwaminifu"

mwenye ulimi wa ukaidi

" hunena kwa ukaidi" au "hunena uovu"

huanguka katika msiba

"atapatwa na msiba"

Proverbs 17:21

moyo mchangamfu ni dawa njema

"moyo mchangamfu ni kama dawa ambayo hukufanya ujisikie vizuri zaidi"

hukausha mifupa

"humfanya mtu awe dhaifu na kukosa afya"

Proverbs 17:23

kwa kupotosha njia za haki

"kwa kuzuia kufanyika kwa haki" au "kwa kuzuia haki"

huelekeza uso wake kwenye hekima

"hutenda kwa busara"

macho ya mpumbavu ni

"mpumbavu ni"

mwisho wa dunia

" hutaza mambo yasiyowezekana"

Proverbs 17:25

mwana mpumbavu ni huzuni kwa baba yake

"mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake"

mwana mpumbavu ...na uchungu kwa mwanamke

mwana mpumbavu...huleta uchungu kwa mwanamke

aliyemzaa

"mzazi wake"

uchungu

hisia za maumivu, huzunu

si vema ..wala si vizuri

"siku zote ni vibaya... na ni uovu"

mtu mwenye haki

"mtu asiyekuwa na hatia,"

kuwachapa

charaza vikali

wenye uadilifu

"ambao ni waaminifu"

Proverbs 17:27

hutumia maneno machache

"husema maneno machache"

hata mpumbavu hufikiriwa kuwa mwenye busara

"watu hudhani hata mpumbavu ni mwenye busara"

hufunga kinywa chake

"haongei"

hudhaniwa kuwa ni mwenye akili

"watu humdhania kuwa ni mwenye akili"

Proverbs 18

Proverbs 18:1

ajitengaye

"kaa mbali na watu wengine"

hupingana na maamuzi yote yaliyosahihi

" huyakataa maamuzi yote yaliyosahihi"

maamuzi sahihi

"maamuzi mema" au "uchaguzi sahihi"

mpumbavu hapati raha katika ufahamu,

mpumbavu huchukui ufahamu na ufurahia katika"

lakini kwa kufunua kilichopo katika moyo wake mwenyewe tu

"lakini kwa kuwaambia wengine kile kilichopo katika moyo wake mwenyewe"

Proverbs 18:3

Dharau huja pamoja naye-sambamba na aibu na shutuma

"huonyesha dharau kwa watu wengine na husabbisha wajisikie aibu na kushutumiwa"

aibu na shutuma

aibu ambayo ama huwakumba watu wengine au mtu mwovu"

maneno ya kinywa cha mtu ni maji yenye kina;... chemchemi ya hekima ni mkondo utiririkao

"maneno yakinywa cha mwenye hekima ni maji yenye kina...chemchemi ya hekima mkondo utiririkao"

maneno ya kinywa cha mtu ni maji yenye kina

"maneno ya kinywa cha mtu ni ya maana sana kama maji yenye kina"

maneno ya kinywa

maneno ya mtu

chemchemi ya hekima ni mkondo utiririkao

"chanzo cha hekima ni tele kama maji ya chemchemi ibubujikayo"

Proverbs 18:5

si vema kwa...kwa mtu mwenye haki

"Ni vema kumtendea mtu mwovu kama anavyositahili, na kutenda haki kwa mtu mwenye haki"

midomo ya mpumbavu huleta

"anasema mtu mpumbavu huleata"

huleta

"husababisha"

kinywa chake hukaribisha mapigo

"kinywa chake husababisha watu kutaka kupiga"

kinywa chake

"maneno yake anayosema"

Proverbs 18:7

kinywa cha mpumbavu ...kwa midomo yake

"ambacho mpumbavu hunena... kwa kile asemacho"

ni uharibifu wake

"ataangamizwa"

hujitega mwenyewe

"atasababisha matatizo kwa ajili yake mwenye"

maneno ya umbeya ni kama chembe mtamu

maneno ya udaku yanafurahisha kusikiliza"

maneno ya umbeya

"maneno ambayo mtu mbeya huongea"

chembe

"vipande vidogo vya chakula"

huzama katika sehemu za ndani ya mwili

"huingia katika akili ya mtu na kuathiri mawazo yake"

Proverbs 18:9

mvivu katika kazi yake ni ndugu yake aliye mharibifu

" anafanana na"

mvivu

"mzembe"

aliye mharibifu zaidi

" mwenye kuharibu kila kitu" au "mwenye uharibifu daima"

jina la Yahwe ni mnara imara

"Yahwe hulinda kama mnara imara" au "Yahwe huwalinda watu wake kama mnara ambao ni imara"

jina la Yahwe

"Yahwe"

wenye haki

"wale ambao hutenda mema" au "watu waadilifu"

huikimbilia na kuwa salama

"hukimbilia kwake na wapo salama" au "wanamtafuta na wapo salama"

Proverbs 18:11

mali ya tajiri ni mji wake wenye ulinzi

"mtu tajiri hutegemea mali yake kama mji unavyotegema ukuta wake"

tajiri

"mtu tajiri"

mji wake wenye ulinzi

mji wenye ulinzi imara kama ukuta na mnara

katika mawazo yake ni kama ukuta mrefu

"hudhani utampatia ulinzi kama ukuta mrefu"

kabla ya anguko lake moyo wa mtu hujivuna

"kwanza moyo wa mtu hujivuna, lakini baadaye huja anguko lake"

anguko

hushuka kwa heshima ya mtu au afya

moyo wa mtu

mawazo na hisia za mtu

unyenyekevu huja kabla ya heshima

"mtu lazima awe mnyenyekevu kabla ya kuweza kuheshimiwa"

Proverbs 18:13

ni upumbavu wake na aibu

"ni upumbavu wake na anapaswa kupata aibu"

roho ya mtu itapona ugonjwa

"mtu mwenye matumaini atapona ujonjwa" au "kama mtu amejaa matumaini ndani yake, ataondokana na ugonjwa"

lakini moyo ulivunjika ni nani anaweza kuusitahimili?

"lakini ni vigumu kusitahimili moyo uliovunjiaka"

moyo uliovunjiaka

kuhuzunika, kuwa na mahuzuniko

Proverbs 18:15

moyo wa mwenye busara hupata

"mwenye busara hutamani kupata"

mwenye busara

"wale wenye busara" au "watu wenye busara"

hupata

"ongeza" au "jipatia"

kusikia kwa mwenye busara hutafua

"mwenye busara huitafuta kujifunza juu ya"

mwenye busara

"watu wenye busara"

huitafuta

hutafuta kujifunza juu ya "maarifa"

huweza kufungua njia

"kutengeneza fursa kwa ajili yake"

humleta mbele

"humwezesha kutambulishwa kwa"

Proverbs 18:17

kwanza

"mtu wa kwanza"

kupiga kura

kuchagua

na kutenganisha washindani imara

"na husababisha washindani kuacha kupigana juu ya ugomvi wao"

Proverbs 18:19

ndungu aliyekosewa ni mugumu kushindwa kuliko mji imara

"kama utamkosea ndugu yako, kutafuta namna ya kupatana naye tena inaweza kuwa vigumu kuliko kupigana kuuteka mji"

ugomvi ni kama makomeo ya ngome

kusulihisha ugomvi ni vigumu kama kuvunja makomeo ya ngome"

ngome

kasri lililozungushiwa uigo/ukuta

tumbo la mtu hujazwa kutokana na matunda ya kinywa chake; kwa mavuno ya midomo yake huridhishwa

" mtu hutoshelezwa kwa matokeo ya mazuri ya mambo anayonena"

matunda ya kinywa chake

"maneno yake mazuri"

tumbo la mtu hujazwa

"mtu hutoshelezwa"

kwa mavuno ya midomo yake

"maneno yake mazuri"

huridhishwa

"hufurahishwa"

Proverbs 18:21

mauti na uzima hutawaliwa kwa ulimi

"ulimi unaweza kuongoza kwenda kwenye uzima au mauti" au "maneno ya watu wanayonena yanaweza kuwaongoza kwenda kwenye uzima au mauti"

kwa ulimi... kupenda ulimi

"kwa maneno ambayo watu huongea ...kupenda kuongea"

watakula matunda yake

"atapokea madhara yake"

Proverbs 18:23

marafiki wengi humleta kwenye uharibifu

"marafiki wengi watamharibu"

huja karibu sana kuliko

"mwaminifu kuliko" au "huwa mwema zaidi"

Proverbs 19

Proverbs 19:1

bora mtu maskini

"ni bora kuwa mtu maskini"

ambaye hutembea katika uadilifu wake

"ambaye huishi katika uadiifu" au "ambaye huishi kwa uaminifu"

ni mpotofu katika kauli

"huongea kwa kupotosha" au "huongea kwa namna mbaya"

kuwa na hamasa bila maarifa

"kufanya kazi kwa bidii bila kujua unachokifanya"

ambaye hukimbia haraka sana hukosea njia

"ambaye hutenda kwa haraka hufanya makosa" au " ambaye hufanya haraka hufanya maamuzi dhaifu"

Proverbs 19:3

moyo wake hukasirika

moyo unawakilisha hisia zake " hughadhabika"

utajiri huongeza marafiki wengi

"wale wenye ukwasi hupata marafiki wengi kwa urahisi"

mtu maskini hutengwa na marafiki zake

"umaskini husababisha mtu kupoteza marafiki zake"

Proverbs 19:5

shahidi wa uongo hatakosa kuadhibiwa

"hakika watamwadhibu shahidi wa uongo"

yeye ambaye hunong'ona uongo hataokoka

"watamkamata mtu yule ambaye hunong'ona uongo"

mtu mkarimi

mtu ambaye mara nyingi hutoa vitu

kila mtu ni rafiki

"huonekana kwamba kila mtu ni rafiki" au "karibia kila mtu ni rafiki"

Proverbs 19:7

jinsi gani rafiki zake huzidi kwenda mbali naye!

"kwa hiyo marafiki zake watamchukia na kujitenga naye"

huyapenda maisha yake mwenyewe

"hujipenda mwenyewe"

ahikaye ufahamu

"mwenye ufahamu"

Proverbs 19:9

shahidi wa uongo hatakosa kuadhibiwa

"hakika watamwadhibu shahidi wa uongo"

hunong'ona uongo

"hudanyanya daima"

haifai

"siyo sawa"

anasa

hali ya ukwasi na furaha

sembuse kwa mtumwa

"haifai zaidi kwa mtumwa" au "ni vibaya zaidi kwa mtumwa"

Proverbs 19:11

Busara humfanya mtu awe mpole

" mtu mwenye busara ni si mwepesi wa hasira"

Busara

angalia 1:4

ni utukufu wake kusamehe

"itakuwa utukufu kwake kusamehe" au "wengine dhani kuwa ni heshima kama atasamehe"

kusamehe

kusahau jambo kwa lengo

ghadhabu ya mfalme ni kama ngurmo ya simba kijana

" ghadhabu ya mfalme ni hatari kama shambulizi la simba kijana"

lakini fadhila yake ni kama umande juu ya majani

"lakini fadhila yake inaburudisha kama umande juu ya majani" au "fadhila yake inaburudisha kama umande juu ya ardhi wakati wa asubuhi"

Proverbs 19:13

ni uharibifu kwa baba yake

"atafanya uharibifu kwa baba yake"

mke mgomvi ni maji ya kutona tona daima

"mke mgomvi anakera na kufadhaisha kama maji yenye kuvuja daima"

mke mgomvi

"mke mbishi" au " mke asiye na makubaliano"

Nyumba na ukwasi ni urithi kutoka kwa wazazi

"watoto hurithi nyumba na mali kutoka kwa wazazi"

busara

angalia 12:23

mke mwenye busara anatoka kwa Yahwe

"Yahwe hutoa mke mwenye busara"

Proverbs 19:15

uvivu humtupa mtu kwenye usingizi mzito

""uvivu humfanya mtu alale sana" au " mtu mvivu hulala sana"

kwenda njaa

"kuwa na njaa"

amri

"amri ambayo alifundishwa"

hulinda maisha yake

"huyatunza maisha yake"

njia zake

"namna anavyoishi "

Proverbs 19:17

yeye ambaye ni mkarimu kwa maskini humkopesha Yahwe

"mtu ambaye hutoa kwa maskini hutoa kwa Yahwe"

maskini

"watu fukara au watu maskini"

wakati kuna matumaini

"wakati bado ni mdogo" au "wakati bado anaweza kufundishwa"

na wala usitamani kumwua

""lakini usimwadhibu sana atakufa" au " kama hutamwadhibu utamwangamiza"

usitamani

"kusudia kumweka"

Proverbs 19:19

mtu mwenye hasira

"mtu ambaye hupata hasira upesi"

lazima alipe malipo ya kosa

" lazima apate madhara ya hasira yake" au "lazima abebe matokeo ya matendo yake wakati wa hasira"

kama utamwokoa

" kama utamaidia baada ya kupata hasira yake ya ghafla"

mara ya pili

"mara mbili" au "tena"

sikiliza ushauri na ukubali maelekezo

haya ni maneno ya kusisitiza umuhimu.

sikiliza

"zingatia ushauri"

Proverbs 19:21

katika moyo wa mtu

"katika akili ya mtu" au "hamasa ya mtu"

kusudi la Yahwe

"mipango ya Yahwe" au "kusudi la Yahwe"

hilo litasimama

Hii ni nahau maanya yake " hilo litatokea"

Proverbs 19:23

Kumheshimu Yahwe huleta uzima kwa watu; kila mmoja wenye nayo atatosheka

"ambao wanamheshimu Yahwe wataishi muda mrefu; mwenye kumheshimu Yahwe atatoshelezwa"

kila mmoja mwenye

"kila anayemheshimu Yahwe"

ametosheka na hana madhara

"atatosheka; atakuwa salama"

mvivu

angalia 10:26

huzika mkono wake katika sinia

"huzamisha mkono wake kwenye sinia" au "huweka mkono wake kwenye sahani". katika utamaduni wa Biblia watu walitumia mikono kula kama watu wengine wanavyofanya hata leo

hataurudisha tena juu kwenye kinywa chake

" lakini ni mvivu kuuleta mkono kwenye kinywa ili kula mwenyewe"

Proverbs 19:25

mpige mwenye dhihaka, na mtu mjinga

"ukimpiga mwenye dhihaka, mtu mjinga"

mpige

"wadhibu"

mtu mjinga

mtu asiye na uzoefu, au "mtu ambaye bado mchanga"

busara

agalia 12:23

mwadibishe mwenye ufahamu, na

"kama utamwadibisha yule mwenye ufahmu"

atapata maarifa

"atajua zaidi"

Proverbs 19:26

huleta aibu na fedheha

"huleta aibu na fedheha kwake mwenyewe" au "huleta kwenye familia yake mwenyewe"

kama utaacha kusikiliza maelekezo

"kama utaacha kuzingatia maelekezo" au "kama utaacha kutii maelekezo"

utapotea

"utaacha" au " au utageuka nyuma"

maneno ya maarifa

"maarifa"

Proverbs 19:28

kinywa cha waovu humeza makosa

"waovu hufurahia kutenda uovu kama wanavyofurahia kula chakula"

kinywa cha waovu humeza makosa

watu waovu wanawakilishwa na "kinywa"

waovu

"watu waovu"

hukumu ipo tayari kwa ajili ya wenye dhuhaka na mapigo kwa ajili

"Yahwe yupo tayari kuwahukumu wenye dhihaka na kuwapiga"

mapigo kwa ajili ya migongo

"mapigo yapo tayari kwa ajili ya migongo"au " yupo tayari kuipiga migongo yao"

mapigo

kuchapa kwa kutumia fimbo au mjeredi

Proverbs 20

Proverbs 20:1

mvinyo ni dhihaka na kileo ni mgomvi

Hapa inaeleza juu ya hatari ya kunywa pombe nyingi

mvinyo ni dhihaka

"mtu ambaye hulewa kwa mvinyo hudhihaki"

kileo ni mgomvi

"mtu ambaye hulewa kwa kileo huanzisha mapinga"

mgomvi

mtu ambaye hupigan kwa makelele, hasa katika sehemu za watu wengi

yeyote ambaye hupotea kwa kunywa hana busara

"anayekunywa hadi kushindwa kufikiri vizuri "

kwa kunywa

"kunywa" hapa inamaanisha kunywa pombe

hana busara

"ni mpumbavu"

kumwogopa mfalme ni kama kumwogopa simba kijana anayeunguruma

ghadhabu ya mfalme hufanya watu waogope kama vile wanakabiliana na simba kijana mwenye kuunguruma"

mwenye kumkasirisha

"kumfanya mfalme akasirike"

hufidia uhai wake

"atakufa"

Proverbs 20:3

ni heshima

"maana yake mtu huyu ataheshimiwa"

kila mpumbavu hurukia kwenye mabishano

"kila mpumbavu huingia kwenye mabishano kwa haraka" au " kila mpumbavu ni mwepesi kujiunga kwenye mabishano"

kulima

kuandaa shamba kwa ajili ya kupanda

wakati wa kupanda

majira ya kupanda

lakini hatapata kitu

"hatapata kitu cha kuvuna"

Proverbs 20:5

kusudio la moyo wa mwanadamu ni kama maji yenye kina

"Ni vigumu kufahamu kusudi katika moyo wa mwanadamu ni kama kufika kwenye kilindi cha kisima" au " kusudi la moyo wa mwanadamu ni vigumu kulifahamu"

mtu mwenye ufahamu

"mtu yule mwenye ufahamu"

atayateka

"atasababisha kusudi kujulikana" au "atalichungu za"

mwaminifu

"mwenye kuaminika"

lakini ni nani anaweza kumpata mtu ambaye ni mwaminifu?

" lakini watu wachache wanaweza mtu ambaye ni mwaminifu" au "lakini ni vigumu kupata mtu ambaye ni mwaminifu kweli "

Proverbs 20:7

hutembea katika uadilifu

"huishi kwa uadilifu wake" au " huishi kwa uamninifu"

mwana wake watafuata baada yake

"mwana wake baada yake"

hupepeta kwa macho yake mabaya yote ambayo yapo mbele yake

"huona na kuchambua maovu ya namna mbalimbali ambayo huletwa mbele yake"

Proverbs 20:9

nani anaweza kusema, " moyo wangu nimeuweka safi; nipo huru kutokana na dhambi zangu"?

"hakuna mtu anaweza kusema kwamba moyo wake ni safi na yupo huru kutoka dhambini"

moyo wangu

"mimi mwenyewe"

safi

mtu ambaye Mungu humtafakari kuwa anakubalika kiroho.

nipo huru kutokana na dhambi zangu

"sina dhambi" au "sijatenda dhambi"

Proverbs 20:11

hata kijana anajulikana kwa matendo yake

"watu wanamjua kijana kwa matendo yake"

mwenendo wake

"matendo yake" au "kwa yale anayotenda"

safi na adili

maneno haya yana maana moja, yanahimiza jinsi kijana alivyo mwema "safi"

masikio ambayo husikia na macho ambayo huona

maana yake ni kwamba Yahwe aliumba milango yetu yote ya fahamu.

Proverbs 20:13

huwa maskini

"anakuwa maskini"

fumbua macho yako

"uwe tayari" au "uwe macho"

"Mbaya! Mbaya!" anasema mnunuzi, lakini akiondoka hujisifu

"Mbaya! Mbaya!" anasema mnunuzi kumkosoa muuzaji, lakini baada ya kununua anakwenda zake akijisifu kuhusu bei ndogo aliyolipa"

Proverbs 20:15

midomo ya maarifa ni marijani ya thamani

"midomo yenye maarifa inathamani kama marijani ya gharama sana"

midomo ya maarifa

"maneno yenye busara" au "maneno ya maarifa"

chukua vazi lake yeye ambaye ameliweka dhamana kwa ajili ya mgeni

"chukua vazi kama dhamana kutoka kwa mdhamini wa mgeni ambaye ameahidi kulipa kwa kitu achoazima mgeni"

ameliweka dhamana

"dhamini kuwa kilichoazimwa kitarudishwa" au "ahidi kulipa deni"

shikilia rehani

" shikilia koti lake kama dhamana ya malipo"

Proverbs 20:17

mkate uliopatikana kwa udanganyifu

"mkate ambao mtu ameupta kwa kudanganya"

kwa udanganyifu

"kwa kuwadanganya wengine"

mkate

"chakula"

ladha yake tamu

" ladha yake ni nzuri"

lakini baadaye kinywa chake kitajaa kokoto

"lakini baadaye ladha yake itakuwa kama kokoto katika kinywa chake" au " lakini punde ladha yake ni kama mchanga katika kinywa chake"

kokoto

vipande vidogo vya jiwe

mipango himarishwa kwa ushauri

"watu huimarisha mipango kwa namna ya ushauri"

Proverbs 20:19

mbeya

maana yake mtu ambaye husengenya sana.

usishirikiane pamoja na

" hupaswi kuwa na urafiki na"

kama mtu atamlaani

"Maana yake kama mtu ataonyesha shaukua ya mambo mabaya yatokee kwa mtu mwingine"

taa yake itazimwa katikati ya giza

"maisha yake tatakoma ghafla kama mwanga ambao umepulizwa katika giza" au "atakufa ghafla"

taa yake itazimwa

"taa yake itazimika"

taa yake

" mwanga wa taa yake"

zimwa

kusababisha mwanga uondoke

Proverbs 20:21

hapo mwanzo

"kabla ya muda"

nitalipiza

"nitakuadhibu"

kumsubiri Yahwe

"kuwa na imani kwa Yahwe" au " kumtumaini Yahwe"

Proverbs 20:23

Yahwe huchukia kipimo visivyo sawa na vipimo vya udhalimu si vizuri

tungo zote mbili zinahusika na jambo moja la kuonyesha "ubaya"

hatua za mtu huogozwa na Yahwe

"Yahwe huongoza hatua za mtu"

hatua za mtu

matendo ya mtu

je kwahiyo anaweza kuifahamu njia yake?

"kwa hiyo mtu hawezi kuifahamu njia yake"

kuifahamu njia yake

"kuifahamu kwa nini mambo kadhaa hutokea katika maisha yake"

Proverbs 20:25

ni mtego

"ni hatari"

kusema kwa haraka

kusema jambo kwa haraka na bila kufikiri kwa umakini maana yake

kuweka nadhiri

"kuweka wakifu kwa Yahwe" au "kutamka kuwa ni takatifu"

kuwapepeta waovu

"kuwatenga waovu"

waovu

"wale ambao ni waovu" au "watu waovu"

na kuwazungushia gurudumu la kupuria juu yao

"na huwaadhibu vikali"

gurudumu la kupuria

"mkokoteni wa kupuria"

Proverbs 20:27

roho ya mtu ni taa ya Yahwe, ikichunguza sehemu zake zote za ndani

"Yahwe anetupatia roho ya kujitambua kwa undani, kama taa inavyokufanya uone katika giza"

agano la uaminifu na dhamana humlinda mfalme

"mfalme hujilinda yeye mwenyewe kwa agano lake la uaminifu na mdhamana"

humlinda mfalme

humweka salama mfalme kutoka katika madhara

kiti chake cha enzi huthibitishwa kwa upendo

kiti chake cha enzi huthibitishwa kwa upendo wake

kiti chake cha enzi huthibitishwa kwa upendo

"mfalme huhakikisha kuwa atatawala kwa muda mrefu kwa kuonyesha upendo kwa wengine"

Proverbs 20:29

mapigo ambayo hujeruhi husafisha mabaya na mapigo husafisha sehemu za ndani

"kumpiga aliyefanya kosa kutamsahihisha na kumfanya kuwa mtu mzuri"

Proverbs 21

Proverbs 21:1

moyo wa mfalme ni mkondo wa maji katika mkono wa Yahwe

"yahwe hutawala moyo wa mfalme kama mtu anavyoyaongoza maji kwa ajili ya umwagiliaji"

moyo wa mfalme

"mawazo ya mfalme na matendo" au" jinsi mfalme anavyofikiri na ambacho anataka kufanya"

kila njia ya mtu ni sawa katika macho yake mwenyewe

"kila mtu hufikiria kwamba anafanya mema"

ni nani huipima mioyo

"ni nani atayahukumu mawazo"

Proverbs 21:3

kutenda haki

"kufanya kila ambacho Yahwe anafikiri kuwa ni haki"

kutenda ...haki

"kuwatendea watu namna Yahwe anavyotaka watu kuwatendea watu wengine"

haki inakubalika zaidi mbele ya Yahwe

"Yahwe anataka zaidi-haki

macho yenye kiburi na moyo wa majivuno

"watu wanaotaka wengine kufikiri kuwa ni bora kuliko watu wengine"

macho yenye kiburi

mtu ambaye anataka watu wengine wafahamu kwamba anafikiri yeye ni bora kuliko wao.

moy wa majivuno

mtu ambaye hufikiri yeye ni bora kuliko wengine

taa ya waovu

"mambo ambayo huwasaidia watu waovu kama taa inavyosaidia kuon kwenye giza"

Proverbs 21:5

bidii

"mtu mwenye bidii" au "mtu ambaye hufanya kazi kwa bidii"

huja katika umaskini

"huwa maskini"

kujipatia utajiri

"kupata utajiri "

mvuke upitao upesi

"umende unaotoweka"

na mtego ambao huua

ambao huvutia wanyama kwenye mtego

Proverbs 21:7

vurugu ya waovu itawasukimia mbali;

Mungu atawaadhibu watu waovu ambao huwaumiza majirani zao wasio kwa sababu ya matendo ya vurugu wanayofanya

vurugu ya waovu

"matendo ambayo waovu hutenda kwa ajili ya kuwaumiza majirani zao wasiokuwa na hatia"

huwasukumia mbali

"kuwakamata na kuwalazimasha kuonekana mbele za Mungu ili aweze kuwahukumu"

njia ya mtu mwenye hatia ni udanganyifu

"mtu mwenye hatia huishi katika njia ya udanganyifu"

danganyifu

"mbaya"

Proverbs 21:9

pembe ya darini

Waisraeli wa kale walitumia muda wao mwingi kwenye dari zao, ambapo ilikuwa baridi zaidi kuliko ndani ya nyumba, na wakati mwingine watu walijenga sehemu ya kutosha kulala katika pembe ya dari

mgomvi

mtu ambaye mara nyingi hubisha au hulalamika

hamu ya waovu ni kutamani ubaya

kutamani

kutamani

"kuwa na hamu kubwa mno"

hakuna huruma machoni pake

"hana huruma" au "ni mchoyo sana"

Proverbs 21:11

mwenye dhihaka anapoadhibiwa

" mtu anapomwadhibu mwenye dhihaka"

mjinga

"bila uzoefu, asiye mkomavu, bado na hali ya uchanga"

mwenye dhihaka

"mtu anayewadhihaki wengine"

mwenye busara anapofundishwa

"mtu anapomfundisha mwenye busara"

hushika maarifa

maarifa yanaongelewa kama ni kifaa ambacho mtu kukisha na kuhifadhi kwa ajili yake.

mwenye haki

"mtu wa haki yeyote" au "Yahwe ambaye ni mwenye haki"

huangalia

" tafakari kwa makini"

watu waovu huleta kwenye maangamizi

"huwaangamiza"

Proverbs 21:13

azibaye masikio yake kwenye kilio cha maskini

Hii ni nahau "ambaye hatasikiliza wakati watu maskini wanapoomba msaada"

hatajibiwa

"hakuna atakayefanya jambo lolote kwa ajili ya kumsaidia"

hutuliza hasira

"kumfanya mtu mwenye hasira ajisikie vizuri na asiendelee kuwa na hasira tena"

Proverbs 21:15

haki inapotendeka

"watawala wanapotenda haki"

huzurura kutoka kwenye njia ya ufahamu

Hii ni nahau "kuacha kuishi kwa busara"

atapumzika katika kusanyiko la wafu

"atabaki katika kusanyiko la roho za wafu"

Proverbs 21:17

ni fidia kwa

"fidia"mtu kuchukua nafasi ya mtu mwingine

mdanganyifu

mtu ambaye huwaumiza wale ambao wanamwami kwa kudanganya na kutenda kwa uongo

watu waadilifu

"watu wenye haki" au " watu waaminifu' au "watu watendao haki"

Proverbs 21:19

busara

"mtu wa busara"

huyaharibu

"huyatumia yote"

Proverbs 21:21

huupima mji

"hupanda juu ya ukuta unaouzunguk mji"

mji wa wenye nguvu

"mji ambao mashujaa wanaishi" au "mji wa mashujaa wenye nguvu"

huuangusha

"huuharibu"

ngome ambayo huitumaini

"kuta na minara kuuzunguka mji ambavyo vilidhaniwa kwamba hakuna mtu angeweza kuvuka kuingia kwenye mji, hivyo walijiona kuwa wapo salama"

Proverbs 21:23

yeye mwenye kulinda kinywa chake na ulimi

"yeye ambaye ni mwangalifu katika maneno anayoyasema"

mtu mwenye kiburi na majivuno...hutenda mambo kwa maringo na ufahari

"watu mwenye kiburi na majivuno hutenda mambo kwa marigo na ufahari"

mwenye kiburi na majivuno

maneno haya yana maana moja kumaanisha jinsi mtu alivyo na kiburi

dhihaka ndilo jina lake

"mwenye dhihaka anapaswa kuitwa "dhihaka"

Proverbs 21:25

uchu wa mvivu humfisha

"mtu mvivu hutaka kukaa bila kazi, na kwa sababu hiyo atakufa" au mtu mvivu atakufa kwa sababu hataki kufanya kazi"

mkono wake hugoma

"yeye hugoma"

hutamani

"taka kitu kwa hamumno" au "kuwa na uchu sana"

hutoa na wala hazuii

"hutoa kila kitu ambacho anapaswa" au "hutoa kwa ukarimu"

Proverbs 21:27

dhabihu ya mwovu ni chukizo

Yahwe huichukia dhabihu ya mwovu.

mwovu

"mtu mwovu" au "watu waovu"

hata ni chukizo zaidi

"Yahwe huichukia zaidi dhabihu"

atasema kwa wakati wote

hii ni kwa sababu watu hawatasahau ambacho amesema

Proverbs 21:29

huufanya uso wake kuwa mgumu

"hujifanya kuwa na ujasiri" au "hatasikiliza kurudiwaiwa"

ni mnyofu katika njia zake

" anauhakika kwamba yale atendayo ni haki kwa sababu huhakikisha ni hakika kabla ya kutenda"

Proverbs 21:30

hakuna hekima, hakuna ufahamu, na hakuna ushauri ambao

"Yahwe ni mkuu kuliko kuliko kitu chochote ambacho mtu anakifahamu, anakifikiri au anachosema. "hakuna mwenye busara, ufahamu wa kitu chochote, au mwenye kuwaagiza wengine kufanya jambo furani"

kusimama dhidi ya Yahwe

"kumshinda yahwe" au " kufanya kazi dhidi ya mapenzi ya Yahwe" au " kuonesha kwamba anahaki na Yahwe amekosea"

farasi hutayarishwa kwa ajili ya siku ya mapigano

"wanajeshi huandaa farasi kwa ajili ya siku ya mapigano"

siku ya mapigano

"wakati kuna mapigano"

Proverbs 22

Proverbs 22:1

jina jema huchaguliwa dhidi ya utajiri mwingi

"mtu anapaswa kuchagua jina jema kuliko utajiri mwingi"

jina jema

"wetu wengine waone ya kuwa ni mtu mwema"

hufanana kwa hili

"wanafanana kwa namna moja" au "wanafanana kwa hili"

Proverbs 22:3

mtu mwenye busara

"mtu ambaye ni mwenye busara" au "mtu mwenye akili njema" angali 12:15

mjinga

"bila uzoefu, asiye mkomavu, bado na hali ya uchanga"

Proverbs 22:5

miiba na mitego huwa katika njia ya mkaidi

wakaidi watapata taabu kwa sababu ya "miiba" ya asili na "mitego" ya kutengenezwa na wanadamu.

mitego

mitambo ya kunasa wanyama

mkaidi

"watu wakaidi"

mwenye kuyalinda maisha yake

"watu ambao wanataka kuishi kwa muda mrefu"

njia anayopaswa kuifuata

"namna ya kuishi"

Proverbs 22:7

kopa ...kopesha

"kopa pesa ...kopesha pesa"

yeye anayepanda udhalimu atavuma taabu

"kama mtu atawatendea kwa udhalimu watu ambao wanauwezo mdogo kuliko yeye, baadaye watamsababishia taabu".

fimbo ya ghadhabu yake itanyauka

  1. mtawala dhalimu atapoteza mamlaka yake ambayo aliyatumia kwa kutenda udhalimu kwa watu. 2)watu watajibu dhidi ya udhalimu wake aliotumia kuwaumiza, na hatakuwa na nguvu ya kuwazuia. "hatakuwa na mamlaka aliyoyatumia kuwaumiza watu"

itanyauka

...miti inapokauka

Proverbs 22:9

mwenye jicho la ukarimu atabarikiwa

"Mungu atambariki mwenye jicho la ukarimu"

mwenye jicho la ukarimu

"mtu mkarimu" au "mtu ambaye yupo tayari kutoa vitu kwa ajili ya watu wengine"

mkate

Mkate ulikuwa chakula kikuu kwa watu wengi nyakati za Biblia, mara nyingi ulitumika kuwakilisha chakila kwa ujumla.

mabishano na matukano vitaondoka

"watu hawatabishana tena au kusema vitu vya kuumizana"

Proverbs 22:11

apendaye usafi wa moyo

" kupenda kuwa na moyo safi" au "kutaka kuwa safi"

huruma

"mpole"

macho ya Yahwe hutazama

"Yahwe huyalinda maarifa"

hutazama maarifa

"huyalinda maarifa"

huyapindua

"huyaharibu"

udanganyifu

"mtu mdanganyifu"

Proverbs 22:13

mtu mvivu husema

"hutoa visingizio ili asifanye kazi"

kinywa cha malaya ni shimo refu

"maneno yasemwayo na malaya yatakuvuta, na utakuwa kama umeangukia kwenye refu na hatari"

malaya

Angalia 5:3

hasira ya Yahwe huchochewa

"Yahwe hukasirika"

hudumbukia ndani yake

"hufanya dhambi kwa sababu ya malaya"

Proverbs 22:15

upumbavu umefungwa katika moyo wa mtoto

"moyo wa mtoto umejaa mambo ya kipumbavu"

fimbo ya adabu

mzazi kutumia namna yoyote ili kuadibisha kama vile kumchapa mtoto kwa fimbo.

huondoa

"itamfanya mtoto kuwa na busara"

kuongeza utajiri wake

"kuwa tajiri" au " kupata pesa zaidi"

kuwapa watu matajiri

"kuwapa pesa watu matajiri"

atakuwa maskini

Nahau "atakuwa maskini"

Proverbs 22:17

Maelezo ya Jumla

Mstari wa 17 unaanza utangulizi wa sehemu mpya ya kitabu cha Mithali

tega sikio lako na usikilize

"sikiliza kwa umakini"

maneno ya busara

"ambayo watu wenye hekima husema"

tumia moyo wako kwa

"fanya bidii kufahamu na kukumbuka"

maarifa yangu

"maarifa niliyonayo, ambayo ninakupatia"

yote yapo tayari kwenye midomo yako

"unaweza kuyaongea muda wowote"

wewe leo

msemaji anasisitiza kuwa maneno haya nanamhusu msikilizaji wala si mtu mwingine

Proverbs 22:20

Maelezo ya Jumla

Mistari hii inaendelea na kukamilisha utangulizi ulianza katika mstari wa 22:17

je sikuandika kwa ajili yako ...wewe?

"unapaswa kufahamu kuwa nimeandika kwa ajili ...yako"

misemo thelathini

katika tafasiri zingine inasomeka "misemo yenye ubora"

kwa wale waliokutuma

maana yake msikilizaji ni mtu ambaye ametumwa na watu kupata habari ya mafundisho na kuwarudishia majibu.

Proverbs 22:22

Maelezo ya Jumla

mistari hii inaanza kueleza juu ya "misemo themathini " 22:20

usimwibie ...kumponda

nyanganya ...dhulumu

maskini

"mtu yeyote ambaye ni maskini" au "watu maskini"

kumponda

saga kuwa unga, maana yake kufanyia dhuluma

mhitaji

'mtu ambaye hana mahitaji kwa ajili ya kuishi"

kwenye lango

sehemu ambapo watu walileta vitu na kuuza na kuamuliwa mambo mbalimbali.

Yahwe atatetea shitaka lao

"Yahwe atawatetea wahitaji kutoka kwa wale wanaowaonea" au ""Yahwea atahakikisha kuwa wahitaji wanapokea haki"

atapokonya uhai wao wale ambao waliwaibia

"atawaangamiza wale ambao wakandamiza watu maskini"

Proverbs 22:24

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

mtu ambaye hutawaliwa na hasira

"mtu asiyeweza kutawala hasira yake"

ghadhabu

kuonesha nguvu nyingi kwa hasira

utakuwa chambo kwa ajili ya nafsi yako

"utakuwa kama mnyama alaye chambo na mtego hujifunga na hujindwa kujiokoa"

chambo kwa ajili ya nafsi yako

"chambo ni kitu ambacho mtu amekiweka ili aweze kukuangamiza"

Proverbs 22:26

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

wapigao mikono

ni kitendo cha kushikana mikono na kuweka agano la makubaliano. Wandishi anaonya juu ya kuweka ahadi ya kulipa deni la mtu.

katika kufanya reheni

"kukubali kulipa kitu ambacho mtu mwingine anadaiwa"

Proverbs 22:28

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

kale

ya zamani sana

jiwe la mpaka

jiwe kubwa ambalo linaonesha ardhi ya mtu mwingine inapokomea na mwanzo wa ardhi ya mtu

baba

wahenga

je unamwona mtu mwenye ujuzi katika kazi yake?

"fikiri juu ya mtu unayemfahamu mwenye ujuzi katika kazi yake"

simama mbele

huwa ni mtumishi wa wafalme na watu wengine wenye vyeo watamtazama kuwa wenye hadhi ya juu na kuhitaji uduma yake.

Proverbs 23

Proverbs 23:1

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

weka kisu kooni mwako

  1. "uwe mwangalifu usile sana" au 2) "usile kitu chochote kabisa"

usitamani

"usishikwe na hamu sana kupitiliza" angalia 21:9

vyakula vizuri

"chakula maalumu na vya gharama"

ni vyakula vya hila

Hii ni nahau "anakupa chakula ili aweze kukudanganya"

Proverbs 23:4

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

usifanye kazi kwa nguvu sana

"usifanye kazi sana kiasi kwamba uwe na uchovu kila siku"

yatamulika juu yake

....kuutamaza utajiri kwa kipindi kifupi

hakika utajiri utajitwalia mabawa kama tai na kuruka juu

"utajiri utapotea kwa haraka kama vile tai anavyoweza kuruka"

mabawa kama tai

mabawa kama mabawa ya tai

Proverbs 23:6

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

mwenye jicho ovu

  1. asiyependa kutoa vitu kwa watu wengine au 2) mtu mwovu

usitamani

"usishikwe na hamu sana kupitiliza" angalia 21:9

vyakula vizuri

"chakula maalumu na vya gharama" angalia 23:1

moyo wake haupo pamoja nawe

Hii ni nahau " Kwa uhalisia hataki ufurahie huo mlo"

utatapiki kile chakula kidogo ulichokula

"utatamani kwamba usingekula kitu chochote"

utakuwa umeharibu sifa zako

"hataweza kufurahi hata kama utasema maneno mazuri juu yake na chakula"

Proverbs 23:9

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

katika masikio ya mpumbavu

"ambapo mpumbavu anaweza kukusikia"

Kale

ya zamani sana

jiwe la mpaka

jiwe kubwa ambalo linaonesha ardhi ya mtu mwingine inapokomea na mwanzo wa ardhi ya mtu mwingine. angalia 22:28

nyang'anya

Maana yake kuanza kutumia ardhi ( au kitu) ambacho ni cha mtu mwingine

yatima

watoto ambao wamefiwa na wazazi

mkombozi wao

Yahwe

atatetea shitaka lao dhidi yako

"atawalinda yatima dhidi yako" au "atahakikisha kuwa yatima wanapokea haki na wewe anakuadhibu"

Proverbs 23:12

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

tumia moyo wako kwa

Hii ni nahau "fanya bidii kufahamu na kukumbuka" pia angalia 22:17

mafundisho

  1. "mambo ambayo watu wanakuambia ni mema na yale mabaya" au 2) "vile watu wanakuambia wanapokusahihisha"

na masikio yako

"tumia masikio yako" au "sikiliza kwa makini"

kwenye maneno ya maarifa

"mimi ninapokuambia ambacho nakijua"

Proverbs 23:13

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

usimnyime mtoto mafundisho

"usipuuze kumfundisha mtoto" au "usikatae kumfundisha mtoto"

usimnyime

kataa kutoa kitu ambacho unajua mtu mwingine anakihitajia

fimbo

"kipande cha mti"

ni wewe unayepaswa kumchapa ... na kuokoa nafsi yake

"wewe ndiye unayepaswa kumchapa...na kuokoa nafsi yake." hakuna mtu mwingine wa kufanya hivyo.

na kuokoa nafsi yake kutoka kuzimu

"na utamlinda na ulimwengu wa wafu" au " utamlinda dhidi ya kifo"

Proverbs 23:15

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

midomo yako inenapo

"wakati usemapo jambo"

Proverbs 23:17

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

isiruhusu moyo wako kuwahusudu wenye dhambi

" usijiruhusu mwenyewe kuwahusudu wenye dhambi" au "hakikisha huwahusudu wenye dhambi"

tumaini lako hataondolewa

"Mungu hataruhusu mtu yeyote kuondoa tumaini lako" au " Mungu atalinda ahadi yake aliyoifanya kwako"

Proverbs 23:19

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

Sikia-wewe! mwanangu

"mwanangu sikiliza kwa makini."

uelekeze moyo wako katika njia

"hakikisha unatenda kwa busara"

walaji wa nyama walafi

  1. watu wanaokula nyama zaidi ya mahitaji yao" au 2) "watu wanaokula chakula kingi zaidi ya hitaji lao."

usingizi utawavika matambara

"kwa sababu wanatumia muda mwingi kwa kula na kunywa,wala hawafanyi kazi kwa hiyo watakuwa maskini"

Proverbs 23:22

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

usimdharau

"onesha adabu kwa"

Inunue kweli, wala usiiuze; nunua hekima, mafundisho, na ufahamu

" Fanya namna yoyote ili uweze kufahamu kweli, uwe na busara, uweze kujifunza namna ya kutenda, ili ufahamu jema na baya; wala usifikirie kitu kingine kuwa ni muhimu zaidi ya haya"

Proverbs 23:24

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

baba wa mtu mwenye haki atafurahi sana, na mwenye kumzaa mtoto mwenye busara atamfurahia

"baba wa mtu mwenye haki, mzazi wa mtoto mwenye busara, atashangilia sana na atamfurahia"

atamfurahia

"atafurahia kwa ajili ya mtoto wake"

Proverbs 23:26

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

nipe moyo wako

"nisikmalaya ilize kwa makini" au "nitumaini kabisa"

macho yako yatazame

" zingatia sana"

malaya...mwanamke mwasherati

Kuna aina mbili za wanawake washerati. "malaya" ni mwanamke ambaye hajaolewa, au "mke wa mume mwingine aliyeolewa. kwa pamoja wanaunda namna ya mwanamke mwasherati.

malaya ni shimo refu

"kulala na malaya ni kama kudumbukia kwenye shimo refu "

malaya

Huyu ni mwanamke ambaye hajaolewa anayefanya mambo ya ngono, wala si wale tu ambao hufanya ngono kwa ajili ya pesa.

shimo refu...kisima chembamba

Sehemu hizi mbili ni rahisi kutumbukia na vigumu kutoka "shimo" kwa sababu ni "refu" na "kisima" kwa kuwa ni "chembamba"

mwanamke mwasherati ni kisima chembamba

"kulala na mke wa mume mwingine ni kama kuangukia ktika kisima chembamba"

kisima

shimo katika ardhi ambalo watu huchimba kwa ajili ya kupata maji

huvizia

kukaa kwa kujificha na kuwa tayari kushambulia mhanga napofika

mdanganyifu

"watu wadanganyifu" au "wale ambao huwadhuru wengine kwa kwa kuwadanganya"

Proverbs 23:29

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

Ni nani mwenye ole? Ni nani mwenye huzuni? Ni nani mwenye mapigano? Ni nani mwenye malalamiko? Ni nani mwenye majeraha bila sababu? Ni nani mwenye macho mekundu?

"Sikilizeni nataka kuwaambia mtu wa ole, huzuni, mapigano, malalamiko, mjeraha bila sababu, na macho mekundu."

macho mekundu

"macho kuwa na rangi nyekundu kama ya damu"

Wale ambao hukawia sana kwenye mvinyo, wale ambao hujaribu kuchanganya mvinyo

Hili ni jibu la maswali ya mstari wa 29. Kuelezea watu ambao hunywa sana mvinyo.

hukawia sana kwenye mvinyo

hutumia muda mwingi kunywa mvinyo na hunywa mvinyo mwingi

kuchanganya mvinyo

  1. kuchanganya aina mbalimbali za mvinyo au 2) vileo vingine ambavyo ni vikali kuliko mvinyo

Proverbs 23:31

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

Mwishoni

"baada ya kunywa"

huuma kama nyoka ...choma kama kifutu

" hukufanya ujisikie vibaya kama umeumwa nyoka au kama kifutu amekuchoma"

kifutu

aina ya nyoka mwenye sumu

moyo wako utasema vitu vya kupotosha

"utafikiri na kuamua vitu vya kupotosha"

vitu vya kupotosha

vitu ambayo Mungu amevitaja kuwa vibaya na viovu ; vitu ambavyo havifai

Proverbs 23:34

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

anayelala juu ya mlingoti

"anayelala juu kwenye ndoo karibu namlingoti"

mlingoti

ufito wa mbao mrefu ambao huwekwe kwenye meli wakati wa safari ya majini

walimpiga ...lakini hakuumia. walinipiga, wala siku hisi kitu

Kwa sababu mtu mlevi hafikirii vizuri, anadhani kuwa watu wanampiga, lakini hasikii maumivu na wala hakumbuki chochote.

nitaamka lini?

mtu mlevi anashangaa ni wakati gani atakuwa na busara tena, wakati madhara ya pombe yatakapoisha.

Proverbs 24

Proverbs 24:1

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

mioyo yao

"wao"

midomo yao

"wao"

huongea juu ya madhara

"huongea jinsi ya kutengeneza(kusababisha ) matatizo"

Proverbs 24:3

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

kwa hekima nyumba hujengwa

"watu wanahitaji kuwa busara kama wanajenga nyumba nzuri"

kwa ufahamu huimarishwa

"watu wanahitaji kufahamu wema na ubaya kama wanataka kuimarisha nyumba"

kuimarisha

"nyumba" inawakilisha familia... familia ambayo huishi kwa amani

Kwa maarifa vyumba hujazwa

"watu wanahitaji kufahamu vitu vya thamani na vizuri kama wanataka kujaza vyumba vyao"

Proverbs 24:5

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

shujaa wa hekima

"shujaa mwenye busara"

mtu mwenye maarifa huongeza nguvu zake

"mtu anayejua mambo mengi ni imara kwa sababu anavijua vitu hivi"

kwa uongozi wa busara

"kama unawatu wenye busara wakikuelekeza jambo la kufanya"

kupigana

"pambana"

washauri

wale ambao huwaambia maafisa wa serikali mambo ya kufanya

Proverbs 24:7

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

juu sana kwa ajili ya mpumbavu

Hii ni nahau " ni vigumu sana kwa mpumbavu kufahamu"

hufumbua kinywa chake

"huongea"

Proverbs 24:8

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

bwana wa njama

" mtu mfitinishaji" au "mchochezi"

Proverbs 24:10

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

nguvu zako ni chache

"unazo nguvu chache sana" au " ni dhaifu kabisa"

Proverbs 24:11

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

wale ambao wanachukuliwa

"wanao wachukua"

wanachukuliwa

"kokotwa kupelekwa mbali"

pepesuka

kutemea upande na karibia na kuanguka. Neno hili linaeleza jinsi mtu anavyotembea anavyokokotwa kupelekwa sehemu.

mchinjaji

"sehemu ambayo watu watauwawa, watawaua kama vile wanavyoua wanyama"

kama unasema,"Tazama...hili",

Mwandishi anajibu jambo ambalo msomaji anaweza kufikiria.

Tazama, sisi

"Tusikilizeni sisi ! hatujafanya chochote kibaya , kwa sababu sisi"

je yeye aupimaye moyo hafahamu usemayo?

"yeye aupimaye moyoanafamu ambacho unasema"

yeye ambaye

" ni Yahwe" au "Yahwe ambaye"

aupimaye moyo

"anajua namna watu wanavyofikiri vyema na hamu zao"

yeye mwenye kuongoza maisha yako, je yeye hajui?

"yeye ambaye huyaongoza maisha yako anayajua"

Je Mungu hatampa kila mmoja kile anachostahili?

"Mungu atampa kila mtu kile anachostahili"

Proverbs 24:13

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

tumaini lako halitakoma

"tumaini lako litaendelea"

Proverbs 24:15

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

usivizie

"kujificha na kusubiri muda utimie"

nyumba yake

nyumba ya mtu mwenye haki

huinuka

"kusimama tena"

watu waovu huangushwa kwa maafa

"Mungu atatumia maafa kuwaangusha watu waovu"

huangushwa

kuangushwa

maafa

wakati ambapo mambo mabaya hutokea kwa watu na mali zao

Proverbs 24:17

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

adui yako huanguka

" jambo baya hutokea kwa adui yako"

moyo wako usifurahi

"usifurahi" " au "jizuie usije ukafuraha"

geuza ghadhabu yake kutoka kwake

"kuacha kuwa na hasira juu yake na kukukasirikia wewe badala yake"

Proverbs 24:19

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

taa ya watu waovu itazimwa

Maisha ya watu waovu itakoma kama taa inavyozimika

Proverbs 24:21

Maelezo ya Jumla

Mistari hii ni mwendelezo wa "misemo thelathini"(22:20)

Hofu

heshima ya kina na utiisho kwa ajili ya mtu mwenye mamlaka

ni nani ajuaye ukubwa wa uharibifu ambao utakuja kwao wote?

"hapana ajuaye ukubwa wa uharibifu ambao utakuja kwao wote?

kwao wote

Maneno haya yanamwakilisha Yahwe na mfalme

Proverbs 24:23

Hii pia ni misemo ya wenye busara

Sentensi hii inaanza mkusanyiko mpya wa mithali

shitaka kwenye sheria

mazingira ya kwenda mbele ya hakimu ambapo kuna mtu anayeshutumiwa kwa kuvunja sheria

Proverbs 24:24

Yeyote asemaye kwa mtu mwovu ...atalaaniwa na watu na kuchukiwa na mataifa

"watu watamlaani yeyote anayemwambia mtu mwovu ...,na watu wa mataifa mengine watamchukia"

mtu mwovu ...mtu mwenye haki

1)watu hawatamwita mtu yeyote mwovu kuwa ni mwenye haki au 2) hakuna mtu atakayesema mtu mwenye hatia ya kosa ni mwenye haki

watapata furaha

"watafurahi sana"

zawadi za wema zitawajia

"watu watawapa zawadi nzuri"

zawadi za wema

"baraka" au "vitu vizuri"

Proverbs 24:26

hubusu midomo

"kuonyesha urafiki wa kweli"

Proverbs 24:28

kwa midomo yako

"kwa yale asemayo"

Nitamlipa

"kufanya kisasi dhidi yake"

Proverbs 24:30

miiba

mimea ambayo haina manufaa yenye miiba miakali

upupu

mimea ambaya imejaa majani yenye kuwasha

ulikuwa umeangushwa

"ulikuwa umeanguka"

Proverbs 24:32

nikapokea mafundisho

"nilijifunza somo"

usingizi kidogo ....kwa kupumzika -na umaskini huja

"unaweza kujisemea mwenyewe, usingizi kidogo ...kwa kupumzika-lakini unasikini utakuja"

umaskini huja juu yako

"umaskini huja juu yako kama mwivi"

mahitaji yako kama askari mwenye silaha

"mahitaji yako yatakuja kwako kama askari mwenye silaha"

Proverbs 25

Proverbs 25:1

kuficha jambo

"kuyahifadhi baadhi ya mambo ya siri"

lakini utukufu

"lakini ni utukufu"

kuchunguza

"hulichunguza jambo" au "hufanya uchunguzi kwa mambo ambayo Mungu ameyaficha"

Kama mbingu ni kwa ajili ya kimo na dunia ni kwa ajili ya kina, ndivyo moyo wa wafalme usivyochunguzika

"Hakuna mtu wenye kuweza kupima kimo cha mbingu au kina cha dunia, hata hakuna mtu anawezakuufahamu moyo wa wafalme"

mbingu

Hii ni jula ya vitu vyote tunavyoviona angani pamoja na jua, mwezi, na nyota.

Proverbs 25:4

takataka

malighafi kwenye chuma ambayo watu ambayo watu huwa hawahitaji na huiondoa kwa kukichoma chuma.

kiti chake cha enzi kitathibitishwa kwa kutenda

"mfalme atathibitisha kiti chake cha enzi kwakutenda" au "atakuwa na mamlaka ya kutawala kwasababu anatenda"

Proverbs 25:6

jitukuze

kumpa mtu heshima.

mfalme

mtu ambaye ni mtawala mkuu wa mji, jimbo au nchi.

Proverbs 25:7

ni bora yeye akuambie, "Njoo huku juu"

maana yake kupelekwa sehemu ya meza ambayo ni karibu na mfalme. "ni bora mtu akukaribishe kukaa karibu na mfalme"

mbele ya mkuu

"mbele ya mtu mkuu"

Maana utafany nini mwishoni wakati jirani yako atakapokuaibisha?

" Maana hutajua ufanye nini mwisho wakati jirani yako atakapukuaibisha" au "Maana kama jirani yako anamaelezo, atakuaibisha, na hutakuwa na kitu cha kusema ili kujitetea mwenyewe."

Proverbs 25:9

hoja yako

"mabishano yako"

usiifunue siri ya mtu mwingine

" usiwashirikishe watu wengine siri ya jirani yako"

na habari mbaya juu yako ambayo haiwezi kunyamazishwa

"wala hutaweza kumzuia kuwaambia wengine mambo mabaya juu yako" au " na atawaambia wengine watu mambo mabaya juu yako na hutakuwa na sifa njema tena"

Proverbs 25:11

Neno linalosemwa katika hali ya kufaani ni tufaha za dhahabu kwenye vyano vya fedha

"Neno linalosemwa kwa wakati sahihi ni zuri kama tufaha za dhahabu kwenye vyano vya fedha"

ufaha za dhahabu kwenye vyano vya fedha

"matunda yaliyopakwa rangi ya dhahabu yaliyowekwa kwenye bakuli la fedha "

Neno linalosemwa

"ujumbe ambao mtu huusema"

pete ya dhahabu au pambo lilitotengenezwa kwa dhahabu safi ndivo alilivyo karipio la busara kwenye sikio lenye kusikiliza

"karipio la busara kwenye sikio lenye kusikiliza ni zuri na la thamani kama pete ya dhahabu au pambo la dhahabu"

sikio lenye kusikiliza

"mtu aliye tayari kusikiliza"

Proverbs 25:13

kama baridi ya theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu

mjumbe mwaminifu anafananishwa na baridi ya theluji kwa sababu vyote hivi ni vizuri.

baridi ya theluji

Hii ni lugha ya picha kuonesha uzuri wa jambo.

theluji

barufu ambayo hudodoka kutoka angani kama mvua

hurejesha uhai wa bwana zake

huwafanya bwana zake walidhoofika na kuchoka kuwa imara na kubrudika tena.

mawingu na upepo bila mvua ndivyo alivyo mwenye kujisifu ...hakutoa

"Mwenye kujisifu ...bila kutoa ni kama mawingu na upepo bila mvua

Proverbs 25:15

Kwa uvumilivu mtawala anaweza kushawishiwa

"Mtu mwenye uvumilivu anaweza kumshawishi mtawala" au "mtu mwenye uvumilivu anaweza kuongea kwa mtawala na kuyabadilisha mawazo yake"

ulimi laini unaweza kuvunja mfupa

"kauli ya upole inaweza kushinda upinza imara"

Proverbs 25:16

Maelezo ya Jumla

mstari wa 16 unaeleza kanuni ya ujumla, na mstari wa 17 hautoi mfano mahususi. Ni sitiari kuonesha kufanya jambo zuri kupita kiasi na kujuta baadaye.

Proverbs 25:18

Mtu ashuhudiaye uongo dhidi ya jirani yake ni kama rungu litumikalo kwenye vita, au upanga, au mshale wenye makali

shahidi wa uongo analinganishwa na silaha ambazo zinaweza kujeruhi au kuangamiza watu

mtu asiyemwaminifu unayemtumaini wakati wa taabu ni kama jino bovu au mguu wenye kuteleza

"Kumtumaini mtu asiye mwaminifu wakati wa taabu kutaleta maumivu kwako kama jino bovu au mguu wenye kuteleza"

Proverbs 25:20

magadi ya soda

haya ni madini ambayo hutoa povu na sauti yanapogusana na asidi kama siki.

huimba nyimbo

"kuimba nyimbo za furaha"

roho nzito

"mtu mwenye huzuni"

Proverbs 25:21

makaa ya moto juu ya kichwa chake

"kusababisha ajisikie hatia kwenye dhamiri na aibu kwa tendo alilofanya"

Proverbs 25:23

upepo wa kaskazini

Katika Israeli upepo kutoka kaskazini maranyi ulileta mvua.

mtu ambaye hunena siri

"mtu mwenye hasira"

hukasirisha nyuso

huwafanya watu wengine wakasirike

pembe ya dari

angalia

mke mgomvi

mke ambaye mara nyingi hubishana na kulalamika

Proverbs 25:25

kama maji ya baridi kwa mwenye kiu, ndivyo ilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali

maji ya baridi yanafananishwa na habari njema maana vyote huburudisha na kufurahisha

kama chemchemi iliyochafuka au bomba lililoharibiwa ndivyo alivyo mtu mwenye haki apepesukapo mbele ya watu waovu

mtu anatarajia kupata maji safi kwenye chemchemi au bomba, ndivyo mwenye haki anapaswa kusimama kwa kile anachokiamini. Hivyo chemchemi au bomba lililoharibika ni kama mwenye haki anayeanguka.

apepesukapo mbele ya watu waovu

  1. kukataa kupambana na watu waovu 2)kujiunga na uovu wao

apepesukapo

"kushindwa kusimama"

mbele ya waovu

"watu waovu wanapomshambulia" au "watu waovu wanapomshawishi kutenda maovu"

Proverbs 25:27

siyo vema kula asali nyingi mno; hivyo ni kama kutafuta heshima baada ya heshima

kupata heshima na kula asali ni vizuri, lakini unaweza kula asali nyingi sana na unaweza kutumia nguvu nyingi ili watu wakuheshimu.

siyo vema

"ni jambo baya"

hivyo ni kama kutafuta heshima baada ya heshima

"ni kufikiria kila wakati jinsi watu wengine wanapaswa kukuheshimu" au "hivyo ni kuongea sifa nyingi sana kwa watu"

mtu asiyejitawala ni kama mji uliobomolewa na usiokuwa na ukuta

Mtu asiyejitawala na mji bila ukuta wote ni dhaifu na wapo katika hatari.

uliobomolewa na usiokuwa na ukuta

"ambao ukuta wake umeangushwa na jeshi na kuharibiwa"

Proverbs 26

Proverbs 26:1

Kama theluji wakati wa joto au mvua kwenye mavuno

"kama ambavyo ingekuwa ni ajabu kuwa na theluji wakati wa joto na mvua kipindi cha mavuno "

hivyo laana isiyositahili haishuki

laana ambayo haimdhuru mtu imeongelewa kana kwamba ni ndege ambaye hatui."laana isiyositahili haitui mahali pake"

laana isiyositahili

"laana kwa mtu ambaye haimstahili"

shuka

tuajuu ya mtu au kitu

Proverbs 26:3

mjeledi ni kwa ajili ya farasi, lijamu kwa ajili ya punda na fimbo ni kwa ajili mgongo wa wapumbavu

mjeledi, lijnamu na fimbo ni vitu ambavyo watu hutumia ilikuwafanya farasi, punda, na wapumbavu wanataka nini.

lijamu kwa ajili ya punda

lijamu imetengenezwa kwa nyuzinyuzi. Watu huweka kwenye vichwa cha punda na kushikilia yuzi moja ili kumfanya punda atembee kama wanavyotaka.

fimbo ni kwa ajili mgongo wa wapumbavu

Nyakati za Biblia watu waliweza kuwacha watoto wao au watumwa wao kwa fimbo ya mti ili kuwatia adabu.

Proverbs 26:5

mjibu mpumbavu na ujiunge katika upumbavu wake

mjibu mpumbavu kulingana na aupumbavu wake " au "mjibu mpumbavu kipumbavu"

hivyo hatakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe

"hivyo hawezi kuwa mwenye busara kwa mtazamo wake" au "hivyo hafikirii wenyewe kuwa ni mwenye busara"

yeye apelekaye ujumbe kwa mkono wa mpumbavu

"yeye anayemtuma mpumbavu kupeleka ujumbe"

hukata miguu yake mwenyewe na kunywa vurugu

"hujiumiza mwenyewe kama mtu anayejikata miguu yake na kunywa vurugu"

kunywa vurugu

vurugu inaonelewa kama kimiminika ambach o mtu anaweza kunywa.

Proverbs 26:7

kama miguu...mithali katika kinywa cha wapumbavu

"mithali katika kinywa cha wapumbavu ni kama miguu ya mtu aliyepooza ambayo kuning'inia"

aliyepooza

mtu ambaye hawezi kutembea au kuhisi chochote katika mwili wake wote.

katika kinywa cha wapumbavu

" katika maongezi ya wapumbavu" au " wapumbavu husema"

kujaribisha jiwe kwenye teo

"jaribishia jiwe kwenye teo ili lisiweze kurushwa"

kutoa heshima kwa mpumbavu

"kumheshimu mpumbavu"

Proverbs 26:9

kama mwiba ...ni methali katika kinywa cha wapumbavu

"mithali katika kinywa cha wapumbavu ni hatari kama mwiba kama unaochoma kwenye mkono wa mlevi"

mwiba ambao unaenda kwenye mkono wa mlevi

kama mtu mlevi anashikilia kichaka chenye miiba, mwiba utamchoma mkononi mwake

katika kinywa cha wapumbavu

"katika kauli ya wapumbavu" au "amba hunena wapumbavu"

amwajiriye mpumbavu

"kumpa kazi mpumbavu"

Proverbs 26:11

kama mbwa kuyarudia matapishi yake

"kama mbwa anavyokula matapishi yake"

Je unamwona mtu ambaye ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe?

" mfikirie mtu ambaye hudhani kwambani mwenye busara lakini hana"

Kuna tumaini zaidi kwa kwa mpumbavu kuliko kwake

"mpumbavu anaweza kuwa na busara zaidi kuliko yeye "

Proverbs 26:13

Mtu mvivu husema , "kuna simba ....katikati ya njia kuu!"

Mtu mvivu hulala na husema kwamb hawezi kwenda nje na kufanya kazi kwa sababu kuna simba njiani au katikati ya njia kuu.

kuna simba njiani

angalia 22:13

bawaba

vipande vya chuma ambavyo huubana mlango kwenye ubao au kitu kingine ili kuweza kufunguka na kufanga

Kama mlango unavyorudi kwenye bawaba zake, ndivy o alivyo mtu mvivu juu ya kitanda chake

Mlango na mtu mvivu huzunguka lakini hawaendi popote.

Proverbs 26:15

huweka mkono wake kwenye sinia

"huweka mkono wake kwenye sinia kula chakula"

hana nguvu kuunyanyua juu kwenye kunywa chake

Hii ni kuonesha uzembe wake. Huuacha mkono wake karibu na chakula lakini hawezi kula chakula.

Mtu mvivu ni mwenye busara zaidi machono pake mwenyewe kuliko watu saba wenye ufahamu

"Mtu mvivu hufikiri ni mwenye busara zaidi kuliko watu saba ambao wanaweza kujibu kwa akili"

Proverbs 26:17

Kama mtu ashikaye masikio ya mbwa, ndivyo alivyo mpitaji ambaye hupata hasira kwenye ugomvi ambao si wake

"mpitaji ambaye hupata hasira kwenye ugomvi wa watu wengine ni kama mtu ambaye hushikilia masikio ya mbwa"

Kama mtu ashikaye masikio ya mbwa

"kama mtu ayemkasirikia mbwa na kumshika masikia yake"

mpitaji ambaye hupata hasira kwenye ugomvi ambao si wake

mpitaji ataanza kubishana na watu waliokuwa wakipigana atawakasirisha na watamuumiza

Proverbs 26:18

kama kichaa ...yule adanganyaye...nakuambia utani?

kichaa na mwogo wote huumiza watu lakini huacha kuwajibika kwa hayo.

nilikuwa nakuambia utani?

"nilikuwa natania tu" au "usinilaumu. Nilikuwa natania tu"

Proverbs 26:20

mbeya

mtu ambaye hupiga sogansana

Mkaa ni kwa ajili ya kuchoma makaa na kuni kwa ajili ya moto

"Kama mkaa unavyosaidia kuchoma makaa na kama kuni zinavyosaidia moto kuwaka"

kuchochea ugomvi

"kusababisha watu wapigane" au "kusababisha watu wabishabe"

Proverbs 26:22

maneno ya umbeya ni kama chembe tamu

"maneno ya umbeya hutamanisha kusikiliza"

hushuka chini katika sehemu za ndani ya mwili

"na huingia katika akili ya mtu na kuyaathiri mawazo yake"

kama rangi ya kioo iliyofunikwa kwenye chombo cha udogo ndivyo vilivyo midomo iwashayo na moyo wa uovu

"Watu wenye midomo ya kuwasha na mioyo ya uovu wapo kamachombo cha udongo kilichofunikwa kwa rangi ya kung'aa"

rangi ya kioo iliyofunikwa kwenye chombo cha udogo

"kioo chenye kungara ambacho hufunika chungu cha udongo"

midomo iwashaya

"kauli yenye hisia" au "kusema vitu vizuri"

moyo wa uovu

"mawazo mabaya" au "tamaa mbaya"

Proverbs 26:24

huficha hisia zake kwa midomo yake

"huficha hisia zake kwa namna anavyoongea" au " huongea kwa jinsi ambayo watu hawawezi kufahamu hisia zake za kweli"

huweka uongo ndani yake mwenyewe

"kwa hila hupanga kuumiza watu"

lakini hamwamini

"lakini haamini kile anachosema"

maana kuna machukizo saba katika moyo wake

"moyo wake umejaa mambo ya chuki" au "maana moyo wake umejaa chuki"

Ingawa chuki yake imefichwa kwa uongo

"ingawa uongo wake umefunikwa kwa chuki" au "Ingawa hufunika chuki yake kwa uongo"

Ingawa chuki yake imefichwa kwa uongo

"Ingawa hudanganya kuhifadhi chuki yake ili watu wasijue" au "Ingawa hudanganya ili watu wasijue ya kuwa anawachukia"

kusanyiko

"jamii ya waisraeli"

Proverbs 26:27

achmbaye shimo atatumbukia ndani yake

"Achimbaye shimo kumtega mtu mwingine atatumbukia mwenyewe"

jiwe litaviringika kurudi kwake yeye anayelisukuma

"mtu akisukuma jiwe ili liviringike chini ya kilima na kumgonga mtu, badala yake jiwe litamrudia yeye"

ulimi udanganyao huwachukia watu unaowajeruhi

"mwogo huwachukia wale ambao huwaumiza kwa uongo wake"

Kinywa chenye kusifia huleta uharibigu

mtu ambaye huwasifu wengine huleta taabu au mtu ambaye huwasifu wengine huababisha uharibifu juu yao

kusifia

tukuza mtu kwa namna isiyofa, kumsifu mtu kwa mambo ambayo si ya kweli

Proverbs 27

Proverbs 27:1

usijifufu kwa ajili ya kesho

"usijisifu kwa ajili ya mipango yako ya kesho"

siku italeta nini

"nini kitatokea katika siku" au "nini kitatatokea kesho"

kinywa chako mwenyewe... midomo yako

"wewe mwenyewe"

mgeni na siyo midomo yako

"mgeni na akusifu na wala siyo midomo yako mwenyewe"

Proverbs 27:3

uchochezi wa mpumbavu ni mzito kuliko vyote

"uchochezi wa mpumbavu ni vigumu kuuvumilia kuliko vyote"

uchochezi wa mpumbavu

"taabu inayosababishwa na mpumbavu" "uchochezi" maana yake maneno ua mtendo yanayosababisha hasira au uchungu

kuna ukatili wenye ghadhabu na mafuriko ya hasira, lakini ni nani anaweza kusimama mbele ya wivu?

"mtu mwenye ghadhabu ni mkatili na mtu mwenye hasira anaogopesha, lakini ni nani anaweza kusimama mbele ya mtu mwenye wivu?

ukatili

ukali"

mafuriko ya hasira

"uharibifu wa hasira"

lakini ni nani anaweza kusimama mbele ya mtu mwenye wivu?

"lakini hakuna awezaye kusimama mbele yake mwenye wivi"

kusimama mbele ya mtu mwenye wivu

"kumzuia mtu mwenye wivu" au "kubakia imara wakati mtu mwenye wivu anapomshambulia"

Proverbs 27:5

bora karipo la wazi

"bora kukemewa katika hali ya wazi"

kuliko upendo wa siri

"kuliko upendo ambao haupo wazi" au "kuliko kupendwa kwa siri"

Mwaminifu ni majeraha yaliyosababishwa na rafiki

"majeraha ambayo husababishwa na rafiki ni mdhamana " maana yake maumivu au huzuni ambayo mtu hupata wakati rafiki yake anapomkemea au kusahihisha.

Mwaminifu ni majeraha yaliyosababishwa na rafiki

"Ingawa huleta huzuni, karipio la rafiki ni la kutegemewa"

lakini adui anaweza kukubusu kwa wingi sana

"busu nyingi za adui ni siyo za kutegemewa" au "adui anaweza kujaribu kudanganya kwa busu maridhawa"

wingi sana

"maridhawa" au "kwa wingi"

Proverbs 27:7

mtu aliyekula na kushiba

"mtu aliyetosheka" au "mtu aliyekula kiasi cha kushiba"

hukataa hata sega la asali

Sega la asali lingetamanisha, lakini si kwa mtu ambaye tayari amekwisha kula na kushiba.

kila kitu kichungu ni kitamu

"kila kitu chenye ladha ya uchungu ni kitamu kwa kuonja"

kama ndege ambaye hutanga tanga kutoka kwenye kiote chake ndiyo alivyo mtu ambaye hupotea ambapo anaishi

"kutanga tanga" na "kupotea" maana yake ni moja kwenye mstari huu

Proverbs 27:9

Marashi

mafuta ya kutamanisha au malihamu

huufanya moyo ufurahi

"humfanya mtu kujisikia furaha"

utamu wa rafiki hutoka katika ukweli wa shauri lake

"tunamthamini rafiki kwa ushauri wake"

nyumba ya ndugu yako

ndugu hapa ni mmoja kutoka katika kabila moja, ukoo, au kundi la watu.

msiba

taabu kubwa au bahari mbaya

Proverbs 27:11

huufanya moyo wangu ufurahi

"hunifanya kujisikia furaha"

kisha nitatoa jibu kwa yule mwenye kunidhihaki

"kisha nitajibu kwa yule anayenidhihaki mimi kwa kumwambia habari yako"

mtu mwenye busara huiona taabu na kujificha mwenyewe, lakini watu wajinga huendela na kuteseka kwa ajili yake

Angalia 22:3

mtu mwenye busara

mtu mwerevu" au "mtu mwenye akili njema"

watu wajinga

"watu ambao hawana uzoefu na hawaja pevuka kifikira"

Proverbs 27:13

chukua vazi la yule ambaye ameweka dhamana kwa ajili ya mgeni

angalia 20:15

ameweka dhamana

angalia 20:15

shikilia rehani

Angalia 20:15

yeye ampaye jirani yake baraka

"kama mtu atampa jirani yake baraka"

hiyo baraka itadhaniwa kuwa ni laana

"jirani atadhania hiyo baraka kuwa ni laana"

Proverbs 27:15

mgomvi

maana yake kuwafanya watu wachukiane kula mmoja au kusababisha mabishano makubwa kati ya watu.

kutona tona daima

"kutona tona kwa mvua daima"

siku ya mvua

siku yenye mvua mfululizo"

kumzuia ni kama kuuzuia upepo, au kujaribu kuyashika mafuta katika mkono wako wa kulia

ni vigumu au haina maana kujribu kumzuia ni kama kujaribu kuuzuia upepo au kushika mfuta katika mkono wako

kumzuia

"kumweka chini ya utawala" au "kumzuia katika ugomvi"

kuuzuia upepo

"kuushikilia upepo" au "au kuudhibiti upepo"

Proverbs 27:17

chuma hunoa chuma; katika njia hiyo hiyo, mtu humnoa rafiki yake

" Kama chuma kinaweza kunoa kipande kingine cha chuma, hivyo tabia ya mtu huendelezwa kwa uongozi wa rafiki yake"

atunzaye

"hudumia, jali"

yeye amlindaye bwana wake ataheshimiwa

"bwana atamheshimu yeye ambaye humlinda"

Proverbs 27:19

moyo wa mtu

" namna mtu anavyofikiri"

mharabu

" mwenye kuharibu"

havishibi

" jaa, tosheka"

macho ya mtu

" matamanio ya mtu"

Proverbs 27:21

kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru kwa ajili ya dhahabu

"kalibu inatumika kusafisha fedha na tanuru hutumika kusafisha dhahabu "

kalibu

Ni kontena linalotumika kupasha joto vitu kwa joto kali

tanuru

jiko ambalo linaweza kuwa moto sana

mtu hujaribiwa wakati wa kusifiwa

"wakati watu wanapomsifu mtu, pia huwa wanampima"

Kama utamtwang mpumbavu ...bado upumbavu wake hautaondoka kwake

Maana yake mpumbavu hata kama atateseka na kuumia atabaki mpumbavu.

mchi

kifaa kigumu chenye ncha ya duara, hutumika kwa ajili ya kutwanga vitu kwenye kinu au bakuli

Proverbs 27:23

hakikisha unafahamu hali ya makundi yako ya kondoo na yajali makundi yako

maneno haya yanaweka msisitizo juu ya kujali

makundi yako ya kondoo

makundi ya kondoo

makundi

makundi ya mbuzi

je taji hudumu kwa vizazi vyote?

"taji haidumu kwa vizazi vyote"

taji

hapa inamaanisha utawala wa kifalme

majani mapya huonekana

"majani mapya huanza kukua"

Proverbs 27:26

Sentensi Unganishi

mistari 26 na 27inakwenda pamoja na mistari 23 hadi 25 kama mithali moja

kondoo watakupa mavazi yako

"sufu za kondoo zitakupa vazi"

mbuzi watakupa thamani ya shamba kwa ajili ya nyumba yako

"ukiuza mbuzi wako watakupa thamani ya shamba"

kwa ajili ya nyumba yako

"kwa ajili ya familia yako yote"

na chakula kwa ajili ya watumishi wsichana

"na kutakuwa na maziwa ya mbuzi kwa chakula cha watumishi wako wasichana"

chakula

chakula

Proverbs 28

Proverbs 28:1

kwa sababu ya uhalifu katika nchi

"kwa sababu ya namna nchi navyokosea"

uhalifu katika nchi

"uhalifu wa watu katika nchi"

kwa mtu mwenye ufahamu na maarifa

" kwa mtu anayefahamu na kujua jinsi ya kutawala"

Proverbs 28:3

dhulumu

"tendea vibaya"

kama mvua inayoshesha ambayo haiachi chakula

mtu maskini wenye kudhulumu watu wengine maskini ni kama mvua ambayo hunyesha kwa nguvu wala haiachi mazao ya kuvuna.

mvua inayonyesha

mvua ya uharibifu

kuiacha sheria

"kuacha sheria ya Mungu"

waishikao sheria

"wale wanaotii sheria ya Mungu"

hupigana dhidi yao

hupingana nao au huwazuia

Proverbs 28:5

watu waovu

"watu watendao mambo mabaya"

hawafahamu haki

"hawafahamu maana ya haki"

wale wamtafutao Yahwe

wale wanaotaka kumjua Yahwe

hufahamu kila kitu

"hufahamu maana ya haki"

bora mtu maskini ...kuliko mtu tajiri

"ni bora kuwa maskini ...kuliko kuwa mtu tajiri"

aendaye kaika uaminifu wake

"huishi kwa uaminifu"

ambaye ni mdanaganyifu katika njia zake

"ambaye si mwaminifu katika yale ayatendayo"

Proverbs 28:7

yeye ashikaye sheria

"yeye ambaye anatii sheria ya Mungu"

mwana mwenye ufahamu

"mwana anayefahamu"

warafi

"watu wanaokula sana"

humwaibisha baba yake

"humtia aibu baba yake"

hufanikiwa

"huongeza utajiri wake"

lipisha riba kubwa

"lipisha pesa ya ziada kwa kukopa"

riba

pesa inayolipwa na mkopaji kwa kutumia pesa ya mtu mwingine

hukusanya utajiri wake

"huleta mali zake pamoja"

kwa mwingine

"mtu mwingine"

huruma

"kumsikitikia mtu mwingine"

Proverbs 28:9

Kama yeye

"kama mtu"

atageuzia mbali sikio lake kuisikia sheria

"atageuzia mbali sikio lake kusikia na kutii sheria"

hata maombi yake ni chukizo

"Mungu anachukia hata maombi yake"

chukizo

angalia 3:31

Yeyote mwenye kumpotosha mwenye haki katika njia mbaya

"Yeyote anayesababisha mwenye haki kwenda katika mwelekeo mbaya"

Yeyote mwenye kumpotosha...njia mbaya ataanguka

"kama mtu yeyote atampotosha...njia mbaya ataanguka"

mwenye haki

"watu wanyoofu"

ataanguka kwenye shimo lake mwenyewe

"ataanguka kwenye mtego ambao ameuchimba"

wakamilifu

"watu wakamilifu"

watapata urithi mzuri

"watarithi kitu kizuri"

Proverbs 28:11

kuwa mwenye busara machoni pake mwenyewe

"kuwa mwenye busara katika mawazo yake mwenyewe" au "kijifikira ni mwenye busara"

mwenye ufahamu

"anayefahamu"

atamchunguza

"ataona asili yake ya kweli"

kunapokuwa na ushindi kwa watu wenye haki

"watu wenye haki wanapofanikiwa"

wainukapo waovu

"wakati waovu wanapopata mamlaka"

waovu

"watu waovu"

watu hujificha wenyewe

"watu huende kujificha"

Proverbs 28:13

huficha dhambi zake

"hufunika dhambi zake "

fanikiwa

"nufaika" au "endelea"

yeye ambaye huziungama na kuziacha atapata rehema

"Mungu ataonesha rehema kwa yule ungama na kuziacha"

yeye ambaye huishi kwa kicho daima amebarikiwa

"Mungu atambariki yule ambaye huishi kwa kicho daima"

huishi kwa kicho

huishi maisha ya kicho

kicho

kumheshimu sana Yahwe na kuonesha kwamba unamtii

mwenye kuufanya mgumu moyo wake

"mtu ambaye huufanya mgumu moyo wake"

kuufanya mgumu moyo wake

"kukataa kumtii Mungu"

ataangukia katika taabu

"ataishia kwenye taabu"

Proverbs 28:15

Kama simba aungurumaye au dubu mwenye hasira ndivyo alivyo mtawala mwovu juu ya watu maskini

watu maskini ambao hawana msaidizi dhidi ya mtawala mwovu ni kama watu ambao simba anawaungurumia na dubu anawashambulia

dubu mweye hasira

dubu ni mnyama mkubwa mwenye manyoya mengi na ni hatari sana, ana makucha na meno makali

mtawala aliyepungukiwa ufahamu

"mtawala ambaye hana ufahamu"

mnyonyaji

mtu ambaye huwatendea watu kwa ukatili na kuyafanya maisha yao kuwa magumu

yeye achukiaye udhalimu

"yeye achukiaye kuwa dhalimu"

huongeza siku zake

huishi maisha marefu

Proverbs 28:17

aliyemwaga damu ya mtu

"aliyeua mtu"

mkimbizi

mtu anyekimbilia mbali kuogopa kuogopa kukamatwa

hadi kifo

"maisha yake yote"

yeye anayekwenda katika uaminifu atakuwa salama

"Mungu atamweka salama mtu ambaye huenenda katika uaminifu"

yeye

mtu yeyote ambaye

anayekwenda katika uaminifu

"huishi kwa uaminifu"

yeye mwenye njia ya udanganyifu

"mtu ambaye haishi kwa uaminifu"

ataanguka ghafula

"ataharibikiwa ghafula" au "ataangamia ghafula"

Proverbs 28:19

hufanya kazi kwenye ardhi yake

maana yake kulima , kupanda na kutunza mazao

yeyote

mtu yeyote

afuataye mambo yasiyofaa

mtu anayeshughulika na mambo ambayo hayazalishi chochote.

atapata umaskini mwingi

"atakuwa maskini sana"

yeye apataye utajiri kwa haraka hatakosa adhabu

"Mungu atamwadhibu yule ambaye hupata utajiri kwa haraka"

yeye apataye utajiri kwa haraka

"yeye anayejaribu kupata utajira kwa haraka"

Proverbs 28:21

kwa kipande cha mkate mtu atafanya ubaya

"mtu atafanya dhambi kwa ajili ya kupata faida kidogo"

fanya ubaya

tenda dhambi

mtu bahili

"mtu mchoyo" Huyu ni mtu ambaye hapendi kutumia mali au pesa yake kwa ushirika na wengine

hufanya haraka kutajirika

mtu bahili huwinda utajiri " ni mroho kwa ajili ya utajiri"

umaskini utakuja juu yake

"ghafula atakuwa maskini"

Proverbs 28:23

yeye amwadibishaye mtu, baadaye atapata kibali kutoka kwake kuliko yule ambaye humsifu kwa ulimi wake

"mtu atakuwa mwenye fadhila kwe aliyemwadibisha kuliko mtu mwenye kumsifu kwa ulimi wake"

yeye amwadibishaye

"kama mtu anaadibisha"

humsifu kwa ulimi wake

"humsifu kwa maneno"

humsifu

kumtukuza mtu kwa namna ambayeo si ya kweli. au kumsifu mtu kwa mambo ambayo si ya kweli

yeye aibaye

"mtu anayeiba"

na husema, "Hiyo si dhambi,"

"na kusema hiyo siyo dhambi"

rafiki wa

"ni mtu wa aina ya "

Proverbs 28:25

mtu mroho

mtu mchoyo anayetaka vitu zaidi, pesa au chakula kuliko mahitaji yake

huchochea mgogoro

"husababisha mgogoro "

yeye nayeutumaini moyo wake

"mtu anyejiamini mwenyewe"

yeyote

"mtu yeyote ambaye"

huenda kwa hekima

"hufuta mafundisho ya busara"

Proverbs 28:27

Mwenye

mtu

maskini

"watu maskini"

hatapungukiwa kitu

" hupata kila kitu anachohitaji"

yeye afumbaye macho yake kwao atapokea laana nyingi

  1. watapokea laana nyingi toka kwa maskini "maskini watatoa laana nyingi kwa yeyote afumbaye macho kwao"au 2"watu watatoa laana nyingi kwa yeyote afumbaye macho yake kwa maskini"

yeye

mtu yeyote

afumbaye macho yake

"asiyejali" au "anayeacha kusaidia"

watu waovu wanapoinuka

"watu waovu wanaposhika mamlaka au utawa katika mamla

huangamia

" huondoka " au "huanguka kutoka kwenye mamlaka" au "huharibiwa"

huongezeka

"huzidi" au "huinuka katika mamlaka"

Proverbs 29

Proverbs 29:1

shupaza shingo yake

"kataa maonyo "

atavunjika katika muda mfupi

"Mungu atamvunja ghafla"

pasipo kupona

"na hakuna mtu ataweza kumsaidia"

watu hushusha pumzi

"watu watakuwa na hofu na huzuni"

Proverbs 29:3

kwa haki

"kwa kutenda haki"

Proverbs 29:5

humsifu jirani yake

humwambia jirani yake mambo ya uongo ili afanye makosa

hutandaza mtego katika miguu yake

"hutega mtego kumnasa mtu huyo"

katika dhambi ya mtu mwovu kuna mtego

Hutamani kufanya mabaya kwa watu wengine, lakini Mungu atayatumia matendo yake hayo kumwadhibu.

Proverbs 29:7

huwasha moto kwenye mji

"huwashawishi watu wa mji kufanya ghasia"

hugeuza ghadhabu

huwafanya watu wenye hasira kuwa na amani

Proverbs 29:9

akibisha na

"kwenda mahakamani dhidi ya "

hughadhabika na kucheka

mpumbavu hukasirika na kumzuia mwenye busaa asiongee

ghadhabika

chukia sana

haptatakuwa na utulivu

"hawataweza kumaliza tatizo"

hutafuta maisha yake

Nahau ambaya maana yake "kutaka kuua"

Proverbs 29:11

huzingatia

"sikiliza" angalia 17:3

maafisa wake wote watakuwa waovu

"ni kana kwamba mtawala anawafundisha maafisa wake kuwa waovu"

Proverbs 29:13

mdhalimu

mtu ambaye huwatendea watu ukatili na kuyafanya maisha yao kuwa magumu

Yahwe huyatia nuru macho yao wote

Hii ni nahau "Yahwe huwapa uzima watu "

kiti chake cha enzi

"ufalme wake"

Proverbs 29:15

fimbo na maonyo hutoa hekima

"kama mzazi atatumia fimbo kwa mtoto wake na kumuonya, mtoto atakuwa na busara"

fimbo

Wazazi walitumia viboko katika Israeli kama vifaa vya kuleta nidhamu kwa kuwachapa watoto wao.

maonyo

kumwambia mtu kuwa jambo analofanya halifai

makosa huongezeka

"watu wengi watafanya makosa na dhambi za zitakuwa mbaya zaidi"

anguko la wale watu waovu

"wale watu waovu huanguka" au "wale watu waovu hupoteza utawala wao"

Proverbs 29:17

yeye ambaye huitunza sheria amebarikiwa

"Mungu atambari mtu yule itunzaye sheria"

Proverbs 29:19

mtumwa hatarekebishwa kwa maneno

"hutaweza kumrekebisha mtumwa kwa kuongea naye"

mtu mwenye haraka katika maneno yake umemtazama?

"unapaswa kutambua kitu ambacho hutoke kwa mtu mwenye haraka katika maneno yake"

Proverbs 29:21

ambaye humdekeza mtumwa wake

"ambaye huruhusu mtumwa wake kuacha kazi na hutendea vema mtumwa wake kuliko watumwa wengine"

mwisho wake

"mtumwa anapokua"

kutakuwa na taabu

mtumwa atakuwa mtu dhaifu

huchochea ugomvi

"husababisha mabishano zaidi kwa watu" Angalia 15:17

bwana wa ghadhabu

"mtu ambaye hupata hasira upesi"

Proverbs 29:23

mwenye roho ya unyenyekevu atapewa heshima

"Yahwe atasababisha watu kumheshimu mwenye roho ya unyenyekevu"

huyachukia maisha yake mwenyewe

"huwa na uadui kwake mwenyewe"

husikia laana na hasemi kitu

"hasemi neno hata baada ya watu kutoa laana juu yake"

Proverbs 29:25

kumwogopa mtu hufanya mtego

"mtu yeyote anayeogopa atakachotendewa na watu ni huwa kama mtego"

mtego

kitanzi ambacho hukamata wanyam kwa kamba

yeye ambaye anamtumaini Yahwe atalindwa

"Yahwe atamlinda yule ambaye anamtumaini"

wengi ambao huutafuta uso wa mtawala

"watu wengi wanataka mtawala wao awajali"

kutoka kwa Yahwe ni haki kwa mtu

Ni Yahwe anayetaka kuona kuwa watu wanatendewa kwa haki

Proverbs 29:27

chukizo

mtu anayepaswa kuchukiwa

Proverbs 30

Proverbs 30:1

Aguri...Yake...Ithiel...ukali

Haya ni majina ya watu

Aguri mwana wa Yake

Aguri ni mtoto halisi wa Yake, wala si mjukuu

kwa Ithiel, kwa Ithiel na ukali

"Hii ni kwa Ithiel, kwa Ithiel na ukali '

Hakika

"kweli" au "Hakuna shaka kwamba"

Mimi sina ufahamu wa wanadamu wala sima maarifa ya Mtakatifu

"Mimi sifahamu chochote ambacho wanadamu wanapaswa kuvifahamu

Proverbs 30:4

Ni nani ...chini?Ni nani...mikono?...Ni nani...kanzu? Ni nani....dunia?

"Hakuna mtu..."

mbinguni

ambako Mungu anaishi

kusanya upepo kwenye uwazi wa mikono yake

"kamata upepo katika mikono yake"

uwazi wa mkono yake

"mkono yake"

kusanya

rundika pamoja vitu vidogo vilivyotawanyika

imarisha miisho ya dunia yote

"ameweka mipaka ya ukomo wa dunia"

Jina lake ni nani, na jina la mwanae ni nani?

"niambie jina lake na jina la mwanae kama unawajua"

Hakika unajua!

"Sidhani kama unamjua mtu anayeweza kufanya mambo hayo"

Proverbs 30:5

limejaribiwa

"ni kama chuma cha thamani ambacho kimetolewa uchafu wote"

yeye ni ngao kwa wale wanaokimbilia kwake

"anawalinda wale wanaokuja kwake na kumwomba awalinde "

kuongeza katika maneno yake

kusema maneno mengine zaidi ya yale aliyosema

utathibitishwa kuwa

"atathibitisha kuwa ume.."

Proverbs 30:7

weka upuuzi na uongo mbali nami

"usiruhusu watu waongee upuuzi na uongo kwangu" au "usiniruhusu kuongea upuuzi na uongo"

upuuzi

uongo, maneno ambyo hana maana

usinipe umaskini wala utajiri

"usiruhusu niwe maskini sana wala tajiri sana"

kama nitapata vingi sana, nitakukataa wewe na kusema

Ni hali ya nadharia, msemaji si tajiri lakini inawezekana kuwa tajiri

kama nitakuwa maskini, nitaiba na kukufuru

Hii inaelezea hali ya nadharia ambayo haijatokea lakini inawezekana mwandishi akawa maskini

nitaiba na kukufuru jina la Mungu

"nitawafanya watu wanaojua kuwa nimeiba vitu wafikiri kuwa hakuna Mungu" au " Nitaharibu heshima ya Mungu kwa kuiba"

Proverbs 30:10

uzushi

kusema uongo juu ya mtu mwingine kwa kusudi la kumuumiza

atakulaani

mtumwa atakulaani

utakuwa na hatia

"watu wataona ni mwenye hatia"

Proverbs 30:11

kizazi ambacho kinalaani ...na hakibariki .....kizazi ambacho ni

"kizazi cha watu wenye kulaani ...na hawabariki ...kizazi cha watu ambao ni "

kizazi

aina au aina au kundi

ni safi machoni pao wenyewe

" huamini kuwa wapo safi"

hawajaoshwa uchafu wao

"Mungu hajawasamehe dhambi zao"

uchafu

takataka , siofaa

Proverbs 30:13

macho yao yameinuka...kope zao zimeinuka juu

watu ambao hudhani kuwa wao ni bora kuliko watu wengine.

kuna kizazi ambacho meno yao ni upanga, na taya zao ni visu, hivyo wanaweza kuwararua maskini ...na wahitaji

Watu wa kizazi ambao huongea vitu vibaya sana ,wanaongelewa mithili ya wanyama mwitu...wanawala maskini na wahitaji

taya

mifupa ya usoni ambapo meno huota

Proverbs 30:15

Mruba anao binti wawili

Huu ni mfano wa kuonesha uroho, kutaka vitu zadi kila mara "Uroho anao binti wawili"

mruba

ni aina ya mnyoo amba huganda kwenye ngozi na kunyonya damu

Wanalia "Nipe na nipe "

" kwa pamoja wote wanaitwa nipe mimi"

kuna vitu vitatu ambavyo havitosheki, vinne ambavyo havisemi "Yatosha"

"Kuna vitu vinne ambavyo havitosheki, ambavyo havisemi, "Yatosha"

ambavyo havitosheki

"daima vinataka zaidi"

ardhi ambayo haitosheki kwa maji

ardhi ambayo haizalishi tena chakula kwa sababu hakuna mvua imeongelewa kana kwamba mtu ambaye hana maji ya kutosha kwa kunywa

beza utiifu kwa mama

"humfikiria mama yake kuwa hana maana na hawezi hata kumtii"

macho yake ...tai

Mwandishi anatoa taswira mbili kwa namna inavyotokea kwa watu wanaofariki wakiwa mbali na makazi ya watu

macho yake yatadonolewa na kunguru wa bondeni

" kunguru wa bondeni watayadonoa macho yake"

kunguru

ndege weusi ambao hula mimea na mizoga ya wanyama

ataliwa na tai

"tai watamla"

tai

moja ya ndege wakubwa ambao hula mizoga ya wanyama

Proverbs 30:18

kuna vitu vitatu ambavyo ni ...vinne ambavyo sivifahamu

"kuna baadhi ya vitu vya kushangaza kwangu ambavyo sivifahamu -vinne ni ":

katika moyo wa bahari

"katikati ya bahari"

Proverbs 30:20

hula na kuufuta mdomo wake

...kufanya uzinzi na kisha kuoga.

Proverbs 30:21

chini ya vitu vitatu dunia hutetemeka, na chini ya vinne haiwezi kuvivumilia

"kuna baadhi ya vitu huifanya dunia kutetemeka, ambavyo haiwezi kuvivumilia, vinne katika hivyo ni:"

mpumbavu anaposhiba chakula

"Mpumbavu mwenye chakula cha kutosha"

mwanamke aliyechukiwa anapoolewa

"mwanamke ambaye watu wanamchukia anapoolewa" au "mwanamke aliyetengwa anapoolewa"

anapochukua nafasi ya bibi yake

anapotawala nyumba(kaya au familia)

Proverbs 30:24

wibari

wanyama wasio na mkia, wana masikio ya duara na miguu mifupi

Proverbs 30:27

mjusi

Reptilia mdogo mwenye miguu minne, mwili mrefu na mkia

Proverbs 30:29

Kuna vitu vitatu ambavyo ni ...vinne ambavyo fahari kwa namna ya kutembea kwake

"kuna baadhi ya vitu ambavyo hutembea kwa fahari. Vinne ya hivi ni :"

fahari

tukufu kama mfalme

jogoo aendaye kwa mikogo

kuku dume ambaye hutembea kwa kujidai

Proverbs 30:32

kusuka

chekecha kwa nguvu

siagi

maziwa ya wanyama ambayo yamesukuwa na kuwa mazito

Proverbs 31

Proverbs 31:1

Mfalme Lemueli

hili ni jina la mfalme

Mwanangu, ni nini? Mwana wa tumbo langu, ni kitu gani? Unataka nini, mwana wa nadhiri zangu?

  1. "unafanya nini"? au " hupaswi kufanya hivyo unavyofanya sasa" 2) "sikiliza ninachokuambia" 3) "usifanye mambo ambayo nitakuonya dhidi yake."

mwanangu...mwana wa tumbo langu... mwana wa nadhiri zangu

msemaji anataka msikiaji atambue na kuheshimu msema anayezungumza.

mwana wa tumbo langu

tumbo linawakilisha mtu

mwana wa nadhiri zangu

  1. nadhiri za ndoa ya mama 2) nadhiri baada ya ndoa yakuwa kama Mungu angeruhusu kupata mtoto angeli mweka wakifu kwa Mungu

usiwape wanamke nguvu zako

"usifanye juhudi sana ili kufanya ngono na wanawake" ama nje ya ndoa au kwa vimada

au njia zako kwa wale ambao huwaharibu wafalme

"au kuruhusu wale ambao huwaharibu wafalme kukushauri"

njia zako

"namna unavyoishi" au "kazi unayofanya"

wale ambao huwaharibu wafalme

labda ni mwanamke malaya

Proverbs 31:4

Lemueli

Hili ni jina la mtu

ambacho kimeamriwa

"ambacho Mungu ameamru" au "ambacho wafalme wameamru wenyewe"

potosha

"badilisha" au " pindisha" au "kana"

Proverbs 31:6

na mvinyo

" na mpe mvinyo"

katika uchungu wa dhiki

"ambao nafsi zao zinauchungu" au "ambao wapo katika mateso"

umaskini wake

"jinsi alivyo maskini"

taabu yake

"mambo mabaya ambayo yanatokea kwake"

Proverbs 31:8

ongea kwa ajili ya wale ambao hawawezi kuongea

"watetee wale ambao hawawezi kujitetea wenyewe"

kwa ajili ya madai ya wote ambao wanaangamia

"hivyo watu watende haki kwa wale wote wanaoangamia"

kwa ajili ya madai

"ongea kwa ajili ya madai" au "ongea kwa niaba ya"

watu maskini na wahitaji

"watu ambao ni mskini hawawezi kupata vitu ambavyo wanahitaji"

Proverbs 31:10

Ni nani anaweza kumpata mwanamke mwema?

"si wanaume wengi wanaoweza kumpata mwanamke mwema"

thamani yake ni kuu kuliko marijani

"anathamani kuliko marijani"

hatakuwa maskini

"daima atapata kile anachohitaji"

Proverbs 31:13

sufu

manyoya ya kondoo ambayo hutumika kutengeneza nguo

kitani

mmea ambao nyuzi zake hutumika kutengeneza nguo ya kitani

kwa furaha ya mikono yake

"hujisikia furaha kufanya kazi kwa mikono yake "

mfanya biashara

mtu anayenunu na kuuza

hugawa kazi kwa ajili ya mtumishi wake wa kike

"huwaambia watumishi wake wa kike kazi ambazo kila mmoja wao anapaswa kufanya kwa siku"

Proverbs 31:16

matunda ya mikono yake

"pesa alizopata"

yeye mwenyewe hujivika nguvu

"hujiandaa yeye mwenyewe kwa kazi nzito"

na huifanya mikono yake kuwa imara

"na huitia nguvu mikono yake kwa kufanya kazi yake"

Proverbs 31:18

huona

"huangalia kwa uangalifu"

usiku wote taa yake haizimika

"huwasha taa usiku kucha anapokuwa akifanya kazi"

kisokotea

fimbo nyembamba yenye ncha ambayo hutumika katika kutengeneza nyuzi

Proverbs 31:20

kwa mkono wake huwafikia maskini

"huwasaidia maskini"

kwa mkono wake huwafikia

angalia 31:18.

huvikwa nguo nyekundu

"nyekundu" haimaanishi rangi ya nguo lakini ni vazi la gharama na lenye joto. "kuwa na mavazi ya gharama na yenye joto "

nyekundu

rangi nyekundu, lakini yenye michirizi ya chungwa.

Proverbs 31:22

kitani

vazi ambalo limetengzwa kwa kitani

mume wake anajulikana

"mume wake anaheshiwa na watu"

anapoketi pamoja na wazee wa nchi

kutengeneza sheria na kusuruhisha kesi

Proverbs 31:24

kitani

vazi lililotengenezwa kwa kitani

mishipi

vipande virefu vya nguo huvaliwa kiunoni au kwenye bega moja

huvikwa nguvu na heshima

"kila mtu anaweza kumwona yupo imara na kwa hiyo wanamheshimu"

huucheka wakati ujao

"haogopi yatakayotekea wakati ujao"

Proverbs 31:26

hufumbua kinywa chake kwa ahekima

"hunena kwa busara"

sheria ya ukarimu ipo kwenye ulimi wake

"huwafundisha watu kuwa na ukarimu"

huangalia njia za nyumba yake

"huhakikisha kuwa familia yake yote inaishi katika njia ambayo inampendeza Mungu"

hawezi kula mkate wa uvivu

"siyo mvivu "

uvivu

kutofanya kazi yoyote na kuwa mzembe

Proverbs 31:28

huinuka na

husimama au hufanyakazi kwa juhudi

humwita aliyebrikiwa

"humpongeza"

umewapita

"umefanya vizuri zaidi kuliko"

Proverbs 31:30

madaha ni udanganyifu

"mwanamke mwenye huruma anaweza kuwadanganya watu" au "mwanamke mwenye tabia njema anaweza kuwa mwovu"

uzuri ni ubatili

"mwanamke ambaye ni mzuri sasa hawezi kuwa mzuri daima"

atasifiwa

"watu watamsifu"

matunda ya mikono yake

"pesa anazopata" angalia 31:13 na 31:16

kazi zake na zimsifu katika malango

"watu wakuu wa mji na wamsifu kwa kazi zake nzuri alizofanya"

Ecclesiastes 1

Ecclesiastes 1:1

Kama mvuke wa ukungu, kama upepo mwanana katika upepo

Hii ni misemo miwili inayomaanisha kitu kimoja na vimeunganishwa kwa ajili ya msisitizo.

Ni faida gani wanadamu huipata ... chini ya jua?

"Binadamu hapati faidi ... chini ya jua."

Ecclesiastes 1:4

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaonesha hali halisi ya mpangilio wa maisha jinsi aelewavyo..

Ecclesiastes 1:7

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaendela na mpangilio halisi wa mtazamo.

Kila kitu huwa uchovu

Kwa kuwa binadamu hawezi kueleza vitu hivi, inakuwa haina maana kujaribu. "kila kitu kinachosha"

Jicho halishibi na kile linachokiona

Mtu hawezi kufikia maelezo rahisi kwa kila anachokiona. "Mtu haridhiki na kile ambacho macho yake yanaona"

wala sikio halishibi na kile linachosikia

Mtu hawezi kufikia maelezo rahisi kwa kila anachosikia. "wala mtu haridhiki na kile ambacho masikio yake yanasikia""

Ecclesiastes 1:9

Taarifa ya Jumla:

Hakuna kitu jipya kuhusu binadamu na shughuli zake.

kila kilichofanyika ndicho kitakachofanyika

"kile ambacho watu wamefanya ndicho ambacho watu watafanya siku za usoni"

Je kuna jambo lolote ambalo watu wanaweza kusema, 'Tazama, hili ni jipya'?

"Hakuna kitu ambacho mtu anaweza kusema, 'Tazama, hiki ni kipya."

nayo hayatakumbukwa

"watu wanaweza wasiyakumbuke pia"

Ecclesiastes 1:12

Nilitia akili yangu

"Nikusudia" au "Niliamua"

kusoma na kutafuta

Misemo hii miwili inamaanisha kitu kimoja na inasisitiza alisoma kwa bidii.

wana wa watu

"binadamu"

matendo yote ambayo yanafanyika

"kila kitu ambacho watu hufanya"

mvuke

"umande" au "pumzi." Haidumu. "cha muda" au "haina maana." Kile ambacho watu wanafanya ni kama umande kwa sababu hakidumu na hakina maana.

kujaribu kuuchunga upepo

Mwalimu anasema kwamba vitu ambavyo watu hufanya ni kama kujaribu kuushika upepo au kuuzuia upepo kupuliza.

Palipopinda hapawezi kunyoshwa! Kisicho kuwepo hakiwezi kuhesabiwa!

"watu hawawezi kunyosha vitu vilivyopinda! Hawawezi kuhesabu kisichokuwepo!"

Ecclesiastes 1:16

nimetia moyo wangu

"Nikusudia" au "Niliamua"

upumbavu na ujinga

Maneno "upumbavu" na "ujinga" yana maana ya kufanana na zinamaanisha kufikiri kwa kijinga na matendo.

kujaribu kuuchunga upepo

Mwalimu anasema kwamba vitu ambavyo watu hufanya ni kama kujaribu kuushika upepo au kuuzuia upepo kupuliza.

Ecclesiastes 2

Ecclesiastes 2:1

Nikasema moyoni

"Nikajiambia"

nitakujaribu kwa furaha

Hapo atakayejaribiwa inamaanisha ni yeye mwenyewe. "Nitajijaribu mwenyewe na vitu vinavyonipa furaha"

Kwa hiyo furahia

"Kwa hiyo nitafurahia vitu vinavyo nipendeza"

Nikasema juu ya kicheko, "Ni wazimu,"

"Nikasema kuwa ni wazimu kucheka wakati mwingine"

Yafaa nini?

"ni batili"

Ecclesiastes 2:3

Nikajipeleleza moyoni mwangu

"Nikawaza sana kuhusu"

kutimiza hamu yangu kwa mvinyo

"kutumia mvinyo kujipa furaha"

Nikaruhusu akili yangu iongozwe na hekima

"Nikawaza kuhusu vitu amabvyo watu wenye hekima walinifundisha"

wakati wa siku za maisha yao

"ili mradi wakiwa hai"

Ecclesiastes 2:4

Nilijenga nyumba kwa ajili yangu na kupanda miti ya mizabibu

Huenda mwandishi aliwaambia watu kuifanya hiyo kazi. "Niliwafanya watu wanijengee nyumba na kunipandia miti ya mizabibu"

bustani na viwanja

Maneno haya mawili yana maana zikukaribiana na zinamaanisha mashamba mazuri ya miti ya matunda.

kumwagilia msitu

"kutoa maji kwa ajili ya msitu"

msitu mahali miti ilikuwa imepandwa

"msitu ambapo miti huota"

Ecclesiastes 2:7

nilikuwa na watumwa waliozaliwa katika ikulu yangu

"watumwa wangu walizaa watoto nao pia walikuwa watumwa wangu"

hazina ya wafalme na majimbo

Hii inamaanisha dhahabu na utajiri mwingine ambao nchi jirani ulilazimishwa kulipa kwa mfalme wa Israeli.

kufurahia kutoka kwa wana wa wanadamu, masulia na wanawake

"Niliwafurahia sana wake wangu wengi na masulia kama mwaname yeyote ambavyo angewafurahia"

Ecclesiastes 2:9

hekima yangu ilikuwa ndani yangu

"nikaendelea kutenda matendo kwa hekima" au "nikaendelea kuwa na hekima"

Lolote ambalo macho yangu yalikitamani

"Chochote nilichoona na kutamani"

sikuyazuia

Hii naweza kuweka katika hali chanya. "nilijipatia"

Sikuuzuia moyo wangu katika furaha yeyote

Hii naweza kuweka katika hali chanya. "Nilijiruhusu kufurahia kila kitu kilichonipa furaha"

moyo wangu ulifurahi

"Nilifurahi"

Ecclesiastes 2:11

matendo yote ambayo mikono yangu iliyokwisha kuyatimiliza

"yote niliyotimiza"

mvuke na kujaribu kuuchunga upepo

walimu anasema kwamba vitu ambavyo watu hufanya ni kama kujaribu kuushika upepo au kuuzuia upepo kupuliza.

upumbavu na ujinga

Maneno "upumbavu" na "ujinga" yana maana ya kufanana na zinamaanisha kufikiri kwa kijinga na matendo.

Kwa maana ni kitu gani mfalme anayekuja baada yangu afanye ... ambacho hakijafanyika?

Mwandishi anatumia swali hili kusisitiza wazo kuwa mfalme ajaye hatawezi kufanya jambo lolote la maana zaidi la yale aliyokwisha yafanye yeye. "Kwa kuwa mfalme ajaye hawezi kufany a kitu ... ambacho tayari hakijafanyika."

mfalme anayekuja ... baada yangu

"mfalme ... anayemridhi mfalme aliyepo." Hii huenda iliandikwa na mfalme aliyekowepo katika utawala, kwa hiyo "baada ya mfalme" inaweza kutafsiriwa "baada yangu"

Ecclesiastes 2:13

hekima ina faida kuliko upumbavu, kama nuru ilivyo bora kuliko giza

hekima ni bora kuliko upumbavu, kama vile nuru ilivyo bora kuliko giza.

Mwenye hekima hutumia macho yake katika kichwa chake kuona mahali anakoenda

"Mtu mwenye hekima ni kama mtu anayetumia macho yake kuona anapoenda"

hutumia macho yake katika kichwa chake

"anaona"

mpumbavu hutembea katika giza

"mpumbavu ni kama mtu anayetembea katika giza"

Ecclesiastes 2:15

nikasema moyoni mwangu

"nikajiambia"

Hivyo kuna utofauti gani kama mimi ni mwenye hekima sana?

Mwandishi anatumia swali kusisitiza wazo lake kuwa hakuna faida ya kuwa na hekima. "Kwa hivyo haina tofauti kama nina hekima sana."

Nikahitimisha moyoni mwangu

"nikahitimisha"

mvuke

"umande" au "pumzi." Haidumu. "cha muda" au "haina maana." Kile ambacho watu wanafanya ni kama umande kwa sababu hakidumu na hakina maana.

mwenye hekima, kama mpumbavu, hakumbukwi kwa muda mrefu

"watu hawatamkumbuka mwenye hekima kwa muda mrefu, kama tu ambavyo hawamkumbuki mpumbavu kwa muda mrefu"

kila kitu kitakuwa kimesahauliwa

"watu watakuwa wamekishwa sahau kila kitu"

Ecclesiastes 2:17

kazi zote zilizofanyika

"kazi zote ambazo watu hufanya"

mvuke na kujaribu kuuchunga upepo

Mwalimu anasema kwamba vitu ambavyo watu hufanya ni kama kujaribu kuushika upepo au kuuzuia upepo kupuliza.

Ecclesiastes 2:19

Na ni nani ajuaye kama atakuwa mwenye hekima au mpumbavu?

"Kwa kuwa hakuna ajuaye kama atakuwa mwenye hekima au mpumbavu."

atakuwa

Hapa inamaanisha mtu yule atakaye rithi utajiri wa Sulemani.

moyo wangu ukaanza kukata tamaa

"Nikaanza kusononeka"

Ecclesiastes 2:21

hatari kubwa

"janga kubwa"

Kwa maana ni faida gani mtu hupata ambaye hufanya kazi kwa juhudi na kujaribu moyoni mwake kutimiza kazi zake chini ya jua?

"Kwa kuwa mtu anayefanya kazi sana na kujaribu moyoni mwake kukamilisha kazi zake chini ya jua hafaidi kitu."

ambaye hufanya kazi kwa juhudi na kujaribu moyoni mwake

Misemo hii miwili inamaana moja na inasisitiza jinsi gani mtu anavyofanya kazi kwa nguvu nyingi.

kujaribu moyoni mwake

"kujaribu kwa wasiwasi"

maumivu na masikitiko

Maneno haya mawili yana maana sawa na yanasisitiza jinsi gani kazi ya mtu ilivyo ngumu.

roho yake haipumziki

"akili yake haipumziki" au "anaendelea kuwa na wasiwasi"

Ecclesiastes 2:24

ukweli huu unatoka kutoka mkononi mwa Mungu

"ukweli huu unatoka kwa Mungu"

Kwa kuwa ni nani anaweza kula au anaweza kupata furaha yoyote tofauti na Mungu?

"Kwa kuwa hakuna awezaye kula au kuwa na furaha yoyote tofauti na Mungu."

Ecclesiastes 2:26

ili kwamba ampe mtu anayempendeza Mungu

Yule amabaye "ampaye" inaweza kumaashiria ni Mungu au mtenda dhambi. Kinachopewa ni kila ambacho mwenye dhambi amekusanya na kutunza. Tafsiri ifuatayo njia moja ya kusema hivi bila kuweka wazi ni nani anayegawa vitu vilivyotunzwa. "ili kwamba yule anayempendeza Mungu awe navyo"

mvuke na kujaribu kuuchunga upepo

Mwalimu anasema kwamba vitu ambavyo watu hufanya ni kama kujaribu kuushika upepo au kuuzuia upepo kupuliza.

Ecclesiastes 3

Ecclesiastes 3:1

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anahama na kuanza kueleza tofauti za maisha.

Kwa kuwa kila kitu na wakati wake, na majira kwa kila kusudi

Misemo hii miwili inamaanisha kitu kimoja na imeunganishwa kuleta msisitizo.

kuzaliwa na ... kufa ... kuua na ... kuponya

Hizi ni sehemu mbali mbali za maisha kama zinavyoelezwa kutoka tofauti moja kabisa hadi nyingine.

wakati wa kung'oa yaliyopandwa

Maana zinazowezekana ni 1) "wakati wa kuvuna" au 2) "wakati wa kutoa magugu" au 3) "wakati wa kung'oa."

Ecclesiastes 3:4

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaendelea na tofauti za maisha.

kulia na ... kucheka ... kuombolezana ... kucheza

Hizi ni sehemu mbali mbali za maisha kama zinavyoelezwa kutoka tofauti moja kabisa hadi nyingine.

Ecclesiastes 3:6

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaendelea na tofauti za maisha.

Ecclesiastes 3:8

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaendelea na tofauti za maisha.

Ni faida gani mfanyakazi aipatayo katika kazi yake?

Hili ni swali la kumfanya mtu kufikiri ili kumelekeza msomaji katika mada yamajadiliano yafuatayo.

Ecclesiastes 3:11

ameweka umilele ndani ya mioyo yao

Hapa "yao" inamaanisha binadamu. "ameweka umilele ndani ya mioyo ya binadamu"

Ecclesiastes 3:12

anapaswa kuelewa jinsi ya kufurahia

Mwandishi anasisitiza zoezi la mtu kufurahia kazi yake, sio ufahamu wa kiakili ya jinsi ya mtu kufurahia kazi yake.

Ecclesiastes 3:14

Chochote kilichopo kimekwisha kuwepo

Hakuna kitu jipya kuhusu binadamu na shughuli zake.

Ecclesiastes 3:16

nimeona ... ubaya upo ... ina ubaya

Misemo hii miwili inamaanisha kitu kimoja na inasisitiza jinsi gani tabia ya uovu ni kawaida.

ubaya upo

"kawaida watu wanapata ubaya"

Nikasema moyoni mwangu

"Nikajiambia"

kila jambo na kila tendo

Misemo hii miwili inamaanisha kitu kimoja na zinaashiria kila tendo wafanyao binadamu.

Ecclesiastes 3:19

Hakuna faida kwa mwanadamu zaidi ya wanyama

"Binadamu hayuko bora zaidi ya wanyama"

kuwa hakuna kila kitu isipokuwa pumzi?

"Kila kitu ni pumzi tu"

Ecclesiastes 3:21

Ni nani ajuaye kama roho ... chini ya nchi?

Mwandishi anadai kuwa wanyama wana roho. "Hakuna ajuaye kama roho ... chini ya nchi."

hakuna lililo jema kwa yeyote zaidi ya

Mwandishi anasisitiza zoezi la mtu kufurahia kazi yake, sio ufahamu wa kiakili ya jinsi ya mtu kufurahia kazi yake.

Ni nani awezaye kumleta ... baada yake?

Hakuna yeyote aliyewahi kumfufua mtu au mnyama kutoka wafu. "Hakuna awezaye kumleta ... baada yake."

Ecclesiastes 4

Ecclesiastes 4:1

Nguvu iko katika mikononi mwa watesaji

"Watesi wao wana mamlaka makubwa"

lakini wateswaji hawana mfariji

Hakuna mwenye mamlaka anayewatetea wanao teswa"

Ecclesiastes 4:2

bahati zaidi kuliko wote wawili ni yule ambaye hajaishi

"yule ambaye bado hajazaliwa ni bora zaidi yao"

Ecclesiastes 4:4

wivu wa jirani ya mtu

Maana zinazowezekana ni 1) Jirani ana wivu na kitu alichounda jirani yake au 2) jirani ana wivu na ufundi alionao jirani yake.

mvuke na kujaribu kuchunga upepo

Hakuna awezaye kuchunga upepo kama vile wanyama. Mwalimu anasema kwamba vitu ambavyo watu hufanya ni kama kujaribu kuushika upepo au kuuzuia upepo kupuliza.

Ecclesiastes 4:5

hukunja mikono yake na hafanyi kazi

kukunja mikono ni ishara ya uvivu na ni njia nyingine ya kusema kuwa mtu amekataa kufanya kazi.

hivyo chakula chake in mwili wake

"matokeo yake ni kusababisha uharibifu wake mwenyewe."

kazi ambayo hujaribu kuuchunga upepo

Sio kila kiza ina faida. Kazi zingine hazina faida kama kuchunga upepo.

Ecclesiastes 4:7

hana mwana, wala ndugu

Mtu huyu hana familia.

macho yake hayatosheki

"haridhiki"

Ninajisumbua na kuharibu furaha yangu kwa ajili ya nani?

"Kuna mtu atakaye faidi kutokana na mimi kufanya kazi kwa bidii na kutofurahi?" au "Kazi yangu hamfaidishi yeyote na sina furaha"

Ecclesiastes 4:9

kama wawili wakilala pamoja, wanaweza kupata joto

Mwandishi anazungumzia watu wawili kupatiana joto kwenye usiku wa baridi.

mtu mmoja anawezaje kupata joto akiwa mwenyewe?

"mtu hawezi kuwa na joto akiwa mwenyewe."

Ecclesiastes 4:12

kusimama katika shambulio

"kujilinda dhidi ya mashambulio"

na kamba ya nyuzi tatu haikatika upesi

kamba yenye meno haikatika kwa wepesi "watu hawawezi kukata kwa wepesi kamba ya meno matatu"

Ecclesiastes 4:13

alizaliwa masikini katika ufalme wake

"alizaliwa kwa wazazi masikini walioishi katika nchi ambayo siku moja atatawala"

Ecclesiastes 4:15

Taarifa ya Jumla:

Badala ya kuchagua vijana wenye hekima, watu wanamchagua mwana wa mfalme ambaye anaweza asiwe na hekima zaidi.

hai na kuzunguka

Maneno "hai" na "kuzunguka" yanamaanisha kitu kimoja na yamewekwa pamoja kwa ajili ya msisitizo.

Hakuna mwisho kwa watu wote

"Kuna watu wengi sana"

mvuke na kujaribu kuuchunga upepo

Mwalimu anasema kwamba vitu ambavyo watu hufanya ni kama kujaribu kuushika upepo au kuuzuia upepo kupuliza.

Ecclesiastes 5

Ecclesiastes 5:1

Nenda kule usikilize

Ni muhimu zaidi kwenda hekaluni kusikiliza na na kujifunza sheria ya Mungu ili kumtii Mungu kuliko kutoa sadaka lakini kuendelea kutenda dhambi dhidi ya Mungu.

Ecclesiastes 5:2

kuongea kwa mdomo wako

Kuweka ahadi au kiapo kwa Mungu.

Usiwe mwepesi sana ... usiufanye moyo wako uwe mwepesi sana

Misemo hii miwili inamaanisha kitu kimoja.

maneno yako yawe machache

"usiseme sana"

Ecclesiastes 5:4

kwa kuwa Mungu hafurahii wapumbavu

Tabia moja ya mpumbavu nikuweka ahadi au viapo ambazo hawana mpango wakutimiza.

Ecclesiastes 5:6

Usiuruhusu mdomo wako kusababisha mwili wako kutenda dhambi

"Usiruhusu kile unenacho kikusababishe utende dhambi"

kwa nini kumfanya Mungu ...mikono

"Itakuwa upumbavu kumfanya Mungu akasirike ... mikono

aharibu kazi ya mikono yako

"aharibu kila kitu ufanyacho"

Kwa kuwa katika ndoto nyingi, kama ilivyo katika maneno mengi, kuna mvuke ubatili

"Kuzidisha maneno haiipi umbo, kama vile kuwa na ndoto nyingi haizifanyi kuwa kweli zaidi."

Ecclesiastes 5:8

masikini akiteswa na kunyang'anywa

"watu kuwatesa watu masikini na kuwaibia"

haki na kutendewa vibaya

Hii inamaanisha aina ya matendo ambayo watu wanastahili. "kutendwa sawa."

usishangae

"usishtuke"

kuna watu katika mamlaka

"kuna watu wenye mamlaka"

hata walio juu yao

Kuna wanaume wengine wana utawala juu ya wanaume walio kwenye madaraka. "wanaume walio na mamlaka zaidi yao"

uzalishaji wa ardhi

"chakula ambacho ardhi inazalisha"

Ecclesiastes 5:10

Huu pia ni mvuke

Kama vile mvuke hauna umbo, vivyo hivo hakuna kuridhika katika kutamani pesa.

Kadri mafanikio yanapoongezeka

"Kadri mtu anavyofanikiwa"

ndivyo wanavyoongezeka watu wanaotumia

Maana zinazowezekana ni 1) "ndivyo mtu anavyotumia pesa zaidi" au 2) "ndivyo pia watukuwepo watu zaidi wakutumia utajiri wake."

Kuna faida gani katika utajiri kwa mmiliki isipokuwa kuutazama kwa macho yake?

"Faida pekee ambayo mmiliki alionao kutokana na utajiri wake ni kwamba anaweza kuutazama tu"

Ecclesiastes 5:12

Usingizi wa mfanyakazi ni mtamu

mtu ambaye anafanya kazi nzuri au ya ukweli anaweza kuridhika akijua alifanya kazi nzuri bila kujali malipo.

kama anakula kidogo au sana

"kama anakula chakula kidogo au chakula kingi"

haumuruhusu yeye kulala vizuri

mtu tajiri haridhiki na utajiri wake. Anabaki macho usiku akiwaza pesa zake. "humweka macho usiku"

Ecclesiastes 5:13

mali iliyowekwa akiba na mwenye nayo

"mwenye mali anatunza utajiri"

kwa bahati mbaya

Maana zinazowezekana ni 1) "kupitia bahati mbaya" au 2) "kwa makubaliano mabovu ya kibiashara."

mwana wake ... habakiziwi chochote mikononi mwake

Hapa usemi "mikononi mwake" inamaanisha umiliki. "haachi mali kwa ajili ya mwana wake"

Ecclesiastes 5:15

mtu azaliwavyo uchi ... ataondoka katika maisha haya akiwa uchi

Kwa kuongezea na kutokua na nguo, neno"uchi" hapa linasisitiza kuwa watu wanazaliwa bila kitu chochote. "mtu yu uchi na hamiliki kitu anapozaliwa ...ataondoka maisha haya kwa njia vivyo hivyo.

ataondoka katika maisha haya

"atakufa"

Hachukui chochote

"hachukui chochote mkononi mwake"

kama mtu alivyo kuja ni lazima aende vivyo hivyo

Hii inamaanisha kuzaliwa na kufa kwa mtu na inaashiria wazo sawa na mstari uliopita.

Hivyo ni faida gani mtu yeyote aipatayo katika kufanya kwa ajili ya upepo?

Mwandishi anatumia swali hili kusisitiza wazo lake kuwa hakuna faida kufanya kazi kwa ajili ya upepo. "Hakuna anayepata faida yoyote kwa kufanyia kazi upepo."

kufanya kwa ajili ya upepo

Maana zinazowezekana ni 1) "kujaribu kuushika upepo" au 2) "kufanyia kazi pumzi apumuayo"

Wakati wa siku zake anakula gizani

Hapa neno "giza" linamaanisha hali ya huzuni. Maana zinazowezekana ni 1) "Wakati wa maisha yake anakula kwa kuomboleza" au 2) "Maisha yake anaishi kwa kuomboleza"

na anafedheheshwa sana na magonjwa na hasira

"na kuteseka sana, kwa kuugua na hasira"

Ecclesiastes 5:18

Tazama

"kuwa makini" au "sikiliza"

kile nilichokiona kuwa kizuri kufaaa

Hapa maneno "kizuri" na "kufaa" zinamaana moja. Ya pili inakazia maana ya ile ya kwanza. "kile nilichokiona kuwa bora zaidi kufanya."

wakati wa siku za maisha haya ambayo Mungu ametupa

"kadri Mungu atakavyo turuhusu kuishi"

wajibu wa mtu

Maana zinazowezekana ni 1) "dhawabu ya mtu" au 2) "fungu la mtu maishani"

Ecclesiastes 5:19

mali na utajiri

Maneno haya mawili yana maana moja. Yanamaanisha pesa na vitu ambavyo anaweza kununua kwa pesa.

kupokea sehemu yake na kufurahi katika kazi yake

Hii inaonesha uwezo wa kuridhika na mtu kufurahia kazi yake.

hakumbuki

Ambaye hakumbuki ni mtu ambaye Mungu amempa zawadi.

siku za maisha yake

"vitu vilivyotokea wakati wa maisha yake.

kuhangaika

"kushughulika"

Ecclesiastes 6

Ecclesiastes 6:1

ni mbaya kwa watu

"inasababisha ugumu kwa watu"

mali na utajiri

Maneno haya mawili yana maana moja. Yanamaanisha pesa na vitu ambavyo anaweza kununua kwa pesa.

hakosi chochote

"ana kila kitu"

Mungu ... hampi uwezo wa kukifurahia

Kukusanya utajiri na mali na kushindwa kuufaidi ni bure.

Huu ni mvuke, teso baya

Mtu kutoweza kufaidi mali yake ni teso baya au laana.

Ecclesiastes 6:3

akizaa watoto mia moja

"akizaa watoto 100"

kuishi miaka mingi, ili kwamba siku za miaka yake ni nyingi

Misemo hii miwili inamaanisha kitu kimoja na imeunganishwa kuleta msisitizo.

moyo wake hautosheki kwa mema

"haridhika na vitu vizuri"

hazikwi kwa heshima

Maana zinazowezekana ni 1)"hakuna atakayemzika" au 2) "hakuna atakayemzika vizuri"

Hata mtoto huyo amezaliwa bila faida

"mtoto wa hivyo amezaliwa bure"

anapita katika giza

Hapa neno "giza" linaweza kumaanisha kati ya dunia ya wafu au kitu ambacho ni kigumu kuelewa. "anakufa bila kuelewa"

jina lake linabaki limefichika

"hakuna ajuaye jina lake"

Ecclesiastes 6:5

ana pumziko ingawa mtu huyo hakupumzika

Mtoto ambaye hakuzaliwa hapitia taabu, anabaki katika mapumziko. wakati mtu aliyeishi miaka mingi bila kuridhika anakosa pumziko.

Hata kama mtu akiishi miaka elfu mbili

Hii ni kukuza neno kuonesha kuwa haijalishi ni muda gani mtu ataishi kama hatafurahia vitu vizuri maishani.

miaka elfu mbili

"miaka 2000"

lakini hajifunzi kufurahia vitu vizuri

Hili ndilo lengo, kuwa mtu anapaswa kufaidi vitu vizuri kutoka katika maisha.

Ecclesiastes 6:7

kujaza mdomo wake

"kuweka chakula mdomoni mwake" au "kula"

hamu yake haishibi

"haridhishi hamu yake"

ni faida gani aliyo nayo mwenye hekima kuliko mpumbavu?

Hekima ya mtu mwenye hekima haimfanyi kuwa na starahe za ziada. "mtu mwenye hekima hada nafuu juu ya mpumbavu."

Ni faida gani aliyo nayo masikini hata kama anajua jinsi ya kutenda mbele ya watu?

"Mtu masikini hana nafuu hata kama anajua kutenda mbele ya watu wengine."

Ecclesiastes 6:9

kile ambacho macho hukiona

Mtu anaweza kuona vitu kwa sababu tayari anavyo. "kile ambacho mtu anacho"

kutamani kile ambacho hamu isiyo tulia inatamani

Hii inamaanisha vitu ambavyo mtu anatamani ila hana. "kutamani kile ambacho hana"

mvuke na kujaribu kuuchunga upepo

Mwalimu anasema kwamba vitu ambavyo watu hufanya ni kama kujaribu kuushika upepo au kuuzuia upepo kupuliza.

Chochote ambacho kimekuwepo

"Watu tayari wameshavipatia majina vitu vilivyopo"

vile mtu alivyo ni kama tayari amekwisha fahamika

"watu tayari wanajua vile binadamu alivyo"

Ecclesiastes 7

Ecclesiastes 7:1

Jina zuri

"Sifa nzuri"

watu wanaoishi ni lazima waweke hili moyoni

Wanahitaji kuzingatia ni aina gani ya jina au sifa waliyonayo na watakayoacha wakifa. "wale walio hai wanapaswa kufikiri kwa makini kuhusu hili."

Ecclesiastes 7:3

uso wa huzuni

Hii inamaanisha kuwa na huzuni. "tukio linalomfanya mtu kuwa na huzuni"

furaha ya moyo

Hapa neno "moyo" linamaanisha mawazo na hisia ya mtu. Furaha inafafanua hali ya hisia ya kuwa mwenye furaha na amani . "kufikiri sawa"

Moyo wa mwenye hekima uko katika nyumba ya maombolezo

"Watu wenye hekima huwaza kwa makini kuhusu kifo"

lakini moyo wa wapumbavu uko katika nyumba ya karamu

"lakini mpumbavu anawazu tu jinsi ya kufurahi"

nyumba ya maombolezo ... nyumba ya karamu

Misemo hii inamaanisha nini kinatokea katika sehemu hizi.

Ecclesiastes 7:5

maonyo ya mtu mwenye hekima

"watu wenye hekima wakikuonya"

kusikiliza wimbo wa wapumbavu

"kusikiliza wapumbavu wakiimba"

kama mlio wa miiba chini ya chungu, ndivyo kilivyo kicheko cha wapumbavu

"kicheko cha wapumbavu" kinalinganishwa na kuchomwa kwa miba ambayo ina kelele ila inateketea upesi.

Ecclesiastes 7:7

Kuchukua kwa nguvu (jeuri)

Hii ina maanisha kumlazimisha mtu kumpa pesa au vitu vingine vya dhamani mtu mwingine ili asimdhuru. Hii inadhaniwa kuwa kosa.

humfanya mtu mwenye hekima kuwa mpumbavu

Maana zinazowezekana ni 1) "humgeuza mtu mwenye hekima kuwa mpumbavu" au 2) "hufanya ushauri wa mwenye hekima kuonekana kama ushauri wa kipumbavu."

huharibu moyo

Hapa neno "moyo" inamaanisha akili. "huharibu uwezo wa mtu kuwaza na kuamua vizuri"

Ecclesiastes 7:8

watu wenye uvumilivu ni bora kuliko wenye majivuno rohoni

Hapo neno "rohoni" inamaanisha mwenedao wa mtu. "watu wenye subira ni bora kuliko watu wenye majivuno" au "tabia ya uvumilivu ni bora kuliko tabia ya majivuno"

Usikasirike haraka rohoni mwako

"Usiwe mwepesi wa hasira" au "Usiwe na hasira kali"

hasira hukaa katika mioyo ya wapumbavu

Hasira inalinganishwa na kitu kinachoishi ndani ya wapumbavu. "watu wapumbavu wamejaa hasira"

Ecclesiastes 7:10

Kwa nini siku za zamani zilikuwa bora kuliko siku hizi?

Mtu anauliza swali hili ili kulalamika kuhusu wakati wa sasa. "Vitu vilikuwa nafuu zamani kuliko sasa"

sio kwa sababu ya hekima kwamba unauliza swali hili

Mtu anayesema maneno haya halinganishi wakati wa sasa na wa zamani kwa mantiki, lakini kulingana na uelewa wake. "ungekuwa na hekima usingeuliza swali hili" au "kuuliza swali hili inaonesha kuwa hauna hekima"

Ecclesiastes 7:11

wale wanaoliona jua

"wale walio hai"

faida ya maarifa ni kwamba hekima humpa uhai

Maana zinazowezekana ni 1) mwandishi anatumia maneno "maarifa" na "hekima" kumaanisha kitu kimoja, au 2) "faida ya kujua hekima ni kwamba inakupa uhai."

humpa uhai kwa yeyote aliye nayo

Inayompa uhai ni hekima. Maarifa na hekima "humpa uhai" kwa njia tofauti. Kuchagua uwekezaji mwema, kuwa na marafiki wazuri, kuchagua hali nzuri ya kuishi kiafya, kuishi kwa amani na wengine ni baadhi ya njia amabvyo hekima "humpa uhai."

Ecclesiastes 7:13

Ni nani awezaye kuimarisha chochote alichokipindisha?

"Hakuna awezaye kunyoosha kitu alichokikunja."

Ecclesiastes 7:14

Wakati nyakati ni njema ... wakati nyakati ni mbaya

"Vitu vizuri vinapotokea ... vitu vibaya vinapotokea"

ishi kwa furaha katika hali hiyo

"uwe na furaha kuhusu vitu hivyo vizuri"

zote ziwepo pamoja

"zote ziwepo kwa wakati mmoja"

chochote kinacho kuja baada yake

Maana zinazowezekana ni 1) "chochote kitakachotokea siku za usoni" au 2) "chochote kitakachotokea duniani baada ya yeye kufa" au 3) "chochote kitakachotokea kwake baada ya kufa."

Ecclesiastes 7:15

licha ya kwamba wana haki

"hata kama wana haki"

mwenye haki katika macho yako mwenyewe

mwenye haki, hekima machoni mwako mwenyewe -Misemo hii miwili inamaanisha kitu kimoja na imeunganishwa kuleta msisitizo.

Usiwe mwenye haki

haki - "Usidhani una haki zaidi ya ambavyo ulivyo"

hekima machoni mwako

"mwenye hekima kwa mawazo yako"

Kwa nini kujiharibu mwenyewe?

Mwandishi anatumia swali kusisitiza kwamba kujiona una haki ni kujiangamiza. "Hakuna sababu ya kujiangamiza."

Ecclesiastes 7:17

Kwa nini ufe kabla ya wakati wako?

"Hakuna sababu ya wewe kufa kabla ya unavyotakiwa"

ushike hekima hii

"jikabidi kwa hekima"

usiache haki iende zake

"usiache kujaribu kuwa mwenye haki" au "unapaswa kuendelea kujaribu kuwa mwenye haki"

atatimiza ahadi zake zote

"atafanya kila kitu ambacho Mungu anatarajia kwake"

Ecclesiastes 7:19

zaidi ya watawala kumi katika mji

Hekima inalinganishwa na watawala wengi wa miji. Hekima inaweza kumfanya mtu kuwa wa muhimu zaidi kuliko watawala wa miji.

anayefanya mema na hatendi dhambi

"anayefanya matendo mazuri na hatendi dhambi"

Ecclesiastes 7:21

kila neno linaongelewa

"kila kitu wanachosema watu"

unafahamu mwenyewe

"wewe mwenyewe unafahamu." Hapa "mwenywe" inatumika kusisitiza "unafahamu."

ndani ya moyo wako

"katika mawazo yako"

Ecclesiastes 7:23

Haya yote nimeyathibitisha

"Hivi vyote amabvyo nimekwisha andaki nimevithibitisha"

ilikuwa zaidi ambavyo ningekuwa

"ilikuwa zaidi ya uwezo wangu kuelewa"

mbali na kina sana

Hekima ilikuwa ngumu kushika. Wakati ulipokuwepo uelewa, ulikuwa mdogo. Ilihitaji utambuzi wa kina zaidi ya vile ambavyo mwandishi aliweza kupata. "ngumu kuelewa"

Ni nani awezaye kuipata?

Mwandishi anatumia swali hili kusisitiza ugumu wa kuelewa hekima. "Hakuna awezaye kuelewa."

Nikageuza moyo wangu

Hapa neno "moyo" inamaanisha akili. "Nikageuza mawazo yangu" au "nikakusudi"

Ecclesiastes 7:26

mwanamke yeyote ambaye moyo wake umejaa mitego na nyavu, na ambaye mikono yake ni minyororo

Mwandishi anasema mwanamke mshawishi ni kama mitego ambayo mwindaji anatumia kushika wanyama.

ambaye moyo wake umejaa mitego na nyavu

Hapa neno "moyo" linamaanisha mawazo na hisia. Huyu ni mwanamke ambaye anajali ya kwake tu. "anayetaka kumtega mtu"

mitego na nyavu

Maneno haya mawili yote yanaonesha njia ambazo watu wanatega wanyama. Anaendelea kufikiria njia za kuwatega wanaume ili wampe vitu.

mikono yake ni minyororo

Hapa neno "mikono" inamaanisha nguvu au mamlaka ya kuongoza. "ambaye hakuna awazaye kutoroka"

mwenye dhambi atachukuliwa naye

"atamkamata mwenye dhambi"

Ecclesiastes 7:27

nikiongeza uvumbuzi mmoja hadi mwingine

"kugundua kitu kimoja baada ya kingine"

ili kwamba nipate ufafanuzi wa ukweli

"ili niweza kufafanua maisha"

mwanamme mmoja mwenye haki miongoni mwa elfu

Mwanamme mmoja tu mwenye haki aliweza kupatikana kati ya wanaume 1,000. "1 mwenye haki kati ya wanaume 1,000"

mwanamke miongoni mwa wale wote

Hakuwepo mwanamke yeyote mwenye haki aliyepatikana katika kundi la wanawake 1,000.

Ecclesiastes 7:29

wametoka katika hali ya unyofu wakitafuta magumu mengi

Maana zinazowezekana ni 1) "wamefanya mipango mingi ya dhambi" au 2) "wamefanya maisha yao wenyewe kuwa magumu."

wametoka

Hapa waliotoka ni wanadamu.

Ecclesiastes 8

Ecclesiastes 8:1

Ni mtu gani mwenye hekima? Ambaye anafahamu matukio yana maana gani katika maisha?

Mwandishi anauliza haya kama maswali yanayoongoza kutoa majibu katika yale atakayoyasema baadaye.

husababisha uso wake kung'ara

Hii inamaanisha kwamba uso wa mtu utaonesha kuwa ana hekima. "inaonekana usoni mwake"

ugumu wa uso wake

"muenekano wake usiopendeza"

Ecclesiastes 8:2

kiapo cha Mungu cha kumlinda yeye

"kiapo ulichoapa mbele za Mungu kumlinda"

Usiharakishe kuondoka mbele ya uwepo wake

Maana zinazowezekana ni 1) usiwe mwepesi kuondoka kimwili katika uwepo wake au 2) kubaki mwaminifu kwa Mfalme, usimuache kwa haraka kwa ajili ya mwingine.

Neno la mfalme hutawala

"Asemacho mfalme ni sheria"

ni nani atakaye mwambia

"hakuna awazaye kumwambia"

Unafanya nini?

"Haupaswi kufanya unachofanya."

Ecclesiastes 8:5

Moyo wa mwenye hekima hutambua

"moyo" unamaanisha mawazo. "Mtu mwenye hekima anatambua"

Ni nani awezaye kumwambia nini kinacho kuja?

Swali hili linasisitiza kuwa hakuna ajuaye kitakachotokea baadaye. "Hakuna awazaye kumwambia kinachokuja."

Ecclesiastes 8:8

Hakuna aliye mtawala wa pumzi yake hata kuizuia pumzi ... hakuna aliye na nguvu juu ya siku yake ya mauti.

Kama vile ambavyo mtu hana uwezo wa kujizuia kupumua, mtu hawezi kuendelea kuishi pale muda wake wa kufa ukifika.

uovu hautawasaidia wale amabao ni watumwa wake

Mwandishi anazungumzia uovu kana kwambani mkuu aliye na watumwa.

nimetia moyo wangu

"Nikusudia" au "Niliamua"

kila aina ya kazi ambayo inafanywa

"kila aina ya kazi ambayo watu hufanya"

Ecclesiastes 8:10

wabaya wakizikwa hadharani

Watu waovu waliokufa walipewa mazishi ya heshima. Inaashiria kuwa miili yao ilipaswa kutupwa katika rundo lililokataliwa la mji au kitu kama hicho. "watu wanawazika waovu hadharani"

Waliondolewa mahali patakatifu na kuzikwa mahali waliposifiwa na watu

"Watu waliwatowa kutoka eneo takatifu na kuwazika na kuwasifu"

Wakati hukumu dhidi ya tendo ovu halihukumiwi haraka

"Wakati watu katika madaraka hawatoi upesi hukumu dhidi ya tendo la uovu"

hushawishi mioyo ya wanadamu

Hapa neno "moyo" linamaanisha mapenzi. "humshawishi binadamu"

Ecclesiastes 8:12

mara mia moja

"Mara 100"

itakuwa vyema kwa wale wanao muheshimu Mungu

"maisha yataenda vyema kwa wale wanaomheshimu Mungu"

wanao mheshimu Mungu, wanaouheshimu uwepo wake

Misemo hii miwili ina maana moja na imeunganishwa kwa ajili ya msisitizo.

maisha yake hayatarefushwa

"Mungu hatarefusha maisha yake"

Siku zake kama kivuli kitowekacho

Maana zinazowezekana ni 1) mwandishi analinganisha urefu wa maisha mtu muovu na kivuli kinachopita upesi au 2) ubora au furaha ya maisha hutoweka kama mtu muovu, hakuna kitu dhabiti katika maisha yake.

Ecclesiastes 8:14

Kuna mvuke mwingine usio faa

"kutokuwa na maana" au "ubatili". Vitu vinatokea ila havipaswi. Kama vile vitu vizuri kuwatokea watu waovu na vitu vibaya kuwatokea watu wema.

jambo jingine linaofanyika juu ya dunia

"kitu kingine ambacho watu wanafanya duniani"

kwa siku zote za maisha yake ambayo Mungu amempa

"kadri Mungu anavyomruhusu kuishi"

Ecclesiastes 8:16

Nikauweka moyo wangu

"Nikusudia" au "Niliamua"

kazi inayofanyika juu ya nchi

"kazi ambayo watu wanafanya duniani"

pasipo kufumba macho

"bila kulala"

kazi inayofanyika chini ya jua

Maana zinazowezekana ni 1) "kazi ambayo Mungu anafanya chini ya jua" au 2) "kazi ambayo Mungu anaruhusu watu kufanya chini ya jua"

Ecclesiastes 9

Ecclesiastes 9:1

nilifikiri haya yote katika akili yangu

"Niliwaza kwa kina sana kuhusu haya yote"

Wote wako katika mikono ya Mungu

Hapa neno "wote" inamaanisha "wenye haki na watu wenye hekima" pamoja na "matendo yao"

mikono ya Mungu

Hapa neno "mikono" linamaanisha nguvu na mamlaka. "chini ya umiliki wa Mungu"

Ecclesiastes 9:2

watu wenye haki na waovu

x

walio safi na wasio safi

x

yeye atoaye dhabibu na yule asiye dhabihu

x

Kama vile watu wema ... wenye dhambi nao watakufa vivyo hivyo

x

yule anayeapa ... vivyo hivyo mtu yule aogopaye kuweka kiapo

x

Ecclesiastes 9:3

kila kitu kinachofanyika

"kila kitu amabacho watu hufanya"

mwisho mmoja

hapa neno "mwisho" linamaanisha kifo.

Mioyo ya wanadamu imejaa uovu, na wazimu uko katika mioyo yao

Hapa neno "mioyo" linamaanisha mawazo na hisia. "Wanadamu wamejaa uovu, na fikra zao ni wazimu"

wanaenda kwa wafu

"wanaenda sehemu ya wafu" au "wanakufa"

Ecclesiastes 9:4

kumbukumbu yao imesahaulika

"watu huwasahau"

Ecclesiastes 9:6

chochote kinachofanyika chini ya jua

"chochote ambacho watu hufanya chini ya jua"

kula mkate wako kwa furaha, na kunywa mvinyo wako na moyo wa furaha

Misemo hii miwili inamaana za kufanana na inasisitiza umuhimu wa kufurahia mambo ya msingi ya maisha.

kula mkate wako kwa furaha

"furahia chakula chako"

kunywa mvinyo wako na moyo wa furaha

Hapa neno "moyo" linamaanisha hisia. "kunywa mvinyo kwa furaha"

Nguo zako ziwe nyeupe siku zote, na kichwa chako kipake mafuta

Kuvaa nguo nyeupe na kupaka kichwa mafuta zilikuwa ishara ya furaha na kusherehekea.

kichwa chako kipake mafuta

"pakaa kichwa chako mafuta"

Ecclesiastes 9:9

Ishi kwa furaha na mwanamke umpendaye

Mtu anapaswa kumpenda mke aliye naye. "Kwa sababu una mke umpendaye, ishi naye kwa furaha"

Chochote mkono wako utakachopata kufanya

"Chochote utakachoweza kufanya"

hakuna kazi, au ufafanuzi au ujuzi au hekima

"wafu hawafanyi kazi au kufafanua au kujua au kuwa na hekima"

Ecclesiastes 9:11

muda na bahati huwaathiri wao wote

"kinachotokea na kitakapotokea huwaathiri wote"

huwaathiri wao wote

Hapa maneno "wao wote" inamaanisha mbio, vita, mkate, utajiri, na upendeleo.

kama vile samaki ... kama ndege ... Kama wanyama, wanadamu

Kifo huwashika wanadamu wakati wasiotarajia, kama vile watu wanavyokamata wanyama wakati wasipotarajia.

katika nyakati mbaya ambazo ghafla huwaangukia

Maana zinazowezekana ni 1) "katika hali mbaya ambayo inawatokea ghafla" au 2) "kwa kifo kinachowapata ghafla."

Ecclesiastes 9:13

katika mji kulikuwa na masikini, mtu mwenye hekima

"katika mji, watu walimkuta mtu masikini mwenye hekima" au "mtu masikini, mwenye hekima aliishi katika mji"

Ecclesiastes 9:16

hekima ya mtu masikini hudharauliwa

Kwa sababu mtu huyu alikuwa masikini, watu hawakuutambua hekima yake, wala kumheshimu kwa hekima yake. "watu husharau hekima ya mtu masikini"

maneno yake hayasikilizwi

Watu waliacha kumsikiliza. "hawasikiliza kile anachokisema" au "hawachukui ushauri wake"

Ecclesiastes 9:17

yanasikiwa vizuri zaidi

"yanaeleweka vizuri zaidi"

Ecclesiastes 10

Ecclesiastes 10:1

Kama nzi walio kufa ... hivyo hivyo upumbavu kidogo

Kama vile ambavyo nzi wanaweza kuharibu manukato, vivyo hivyo upumbavu unaweza kuharibu sifa ya mtu kwa hekima na heshima.

Moyo wa mtu mwenye hekima ... moyo wa mpumbavu

Hapa neno "moyo" inamaanisha akili na nia. "Jinsi mtu mwenye hekima anavyowaza ... jinsi mpumbavu anavyowaza"

huelekea kulia ... huelekea kushoto

Hapa maneno "kulia" na "kushoto" yanamaanisha yalio sawa na yasiyo sawa. "hufanya yaliyo sawa .. hufanya yasiyo sawa"

fikira zake zina upungufu

"ni mjinga"

Ecclesiastes 10:4

Kama jazba za mtawala zikiinuka kinyume na wewe

"kama mtawala akiwa na hasira na wewe"

Ecclesiastes 10:5

Wapumbavu wanapewa nafasi za uongozi

"Watawala wanawapa wapumbavu nafasi za uuongozi"

watu walio fanikiwa wanapewa nafasi za chini

"wanawapa nafasi za chini watu waliofanikiwa"

Ecclesiastes 10:8

Taarifa ya Jumla:

Kazi haikosi hatari.

anaweza kuumizwa nayo

"mawe hayo yanaweza kumuumiza"

Ecclesiastes 10:10

Taarifa ya Jumla:

Mithali kidogo

hekima hutoa faida kwa mafanikio

Mtu mwenye hekima angenoa bapa lake na asingelazimika kufanya kazi sana.

kabla hajafurahi

"kabla anayechezea nyoka hajamchamsha"

Ecclesiastes 10:12

Taarifa ya Jumla:

Mithali inaendelea.

Maneno ya kinywa cha mtu mwenye hekima yana huruma

"Vitu ambavyo mtu mwenye hekima husema vina huruma"

midomo ya mpumbavu humumeza mwenyewe

Hapa neno "kumeza" inaashiria kuteketeza. "Vitu ambavyo mtu mpumbavu hunena humteketeza"

Ecclesiastes 10:13

Kama maneno yanavyo anza kutiririka mdomoni mwa mpumbavu

"Kama mpumbavu anavyoanza kuongea"

mwisho mdomo wake hutiririka wazimu mbaya

"anapomaliza kuonge, anaongea wazimu mbaya"

Mpumbavu huongeza maneno

"Mpumbavu huendelea kuongea"

hakuna ajuaye kinachokuja

Swali hili linasisitiza kuwa hakuna ajuaye kitakachotokea baadaye. "Hakuna awazaye kumwambia kinachokuja."

Ni nani ajuaye baada yake?

Mwandishi anauliza hili swali kusisitiza kuwa hakuna ajuaye kitakachotokea baadaye. "Hakuna ajuaye kitakachokuja baada yake."

Ecclesiastes 10:15

huwachosha

"huwasababisha kujisikia uchovu"

hata hawajui barabara ya kwenda mjini

Maana zinazowezeka ni 1) kwamba mtu mpumbavu anachoka sana kutokana na kufanya kazi sana hadi anashindwa kujua njia ya kwenda popote, au 2) kwamba mtu mpumbavu anachoka kutokana na kufanya kazi sana kwa sababu hajui ya kutosha kwenda nyumbani.

Ecclesiastes 10:16

Ole wako ardhi ... umebarikiwa ardhi

Katika mstari huu, mwandishi anazungumza na taifa kana kwamba ni mtu.

kama mfalme wako ni kijana mdogo

Hii inamaanisha kuwa mfalme hana uzoefu au hajapevuka kiakili. Lakini tafsiri zingine za kisasa zinatafsiri neno la Kihebrania kama "mtumishi"

huanza karamu ahsubuhi

Hii huashiria kuwa viongozi wanajali zaidi kuwa na wakati mzuri kuliko kuongoza taifa.

mfalme wako ni mwana wa waungwana

Hii huashiria kuwa mwana huyu amefundishwa vizuri na wakubwa wake katika desturi za kuwa mfalme mzuri.

Ecclesiastes 10:18

Kwa sababu ya uvivu paa huanguka

Mtu mvivu hawezi kuitunza nyumba kwa kawaida.

kwa sababu ya mikono isiyo fanya kazi

"kwa sababu ya mtu asiye fanya kazi"

Watu huandaa chakula kwa ajili kicheko

"Watu huandaa chakula kwa ajili ya kucheka"

divai huleta furaha maishani

"divai husaidia watu kufurahia maisha"

fedha hutimiza hitaji kwa kila kitu

Maana zinazowezekana ni 1) "fedha husaidia kila hitaji" au 2) "fedha husaidia kwa ajili ya chakula na divai."

Ecclesiastes 10:20

hata katika akili

"hata katika mawazo yako"

wenye mali katika chumba chako

"watu matajiri ukiwa chumbani mwako." Hii inamaanisha usiwalaani watu matajiri hata katika sehemu yako ya faragha ambapo hakuna yeyote atakayekusikia.

Kwa kuwa ndege wa angani ... kinaweza kusambaza jambo

Mistari hii miwili inamaanisha kitu kimoja na imeunganishwa kwa ajili ya msisitizo. Mwandishi unatumia sitiari ya ndege kusema kuwa watu watajua ulichosema kwa njia moja au nyingine.

Ecclesiastes 11

Ecclesiastes 11:1

Peleka mkate wako juu ya maji, kwa kuwa utaupata tena baada ya siku nyingi

Maana zinazowezekana ni 1) kuwa mtu anapaswa kuwa mkarimu na mali yake na kisha atapokea ukarimu kutoka kwa wengine (UDB), au 2) kuwa mtu anapaswa kuwekeza mali zake ng'ambo na atapata faida humo.

Shiriki mkate na watu saba, hata wanane

Maana zinazowezekana ni 1) kugawana mali zako na watu wengi, au 2) kuwekeza mali zako sehemu nyingi.

saba, hata wanane

"7, hata 8" au "wengi"

majanga gani yanayo kuja juu ya nchi

Hapa msemo "juu ya nchi" inamaanisha "duniani" au "katika jamii."

yanajivua yenyewe chini ya nchi

Hapa neno "nchi" inamaanisha "katika ardhi."

kuelekea kusini au kuelekea kaskazini

"katika upande wowote"

Ecclesiastes 11:4

Yeyote autazamaye upepo yawezekana asipande

Maana zinazowezekana ni 1) "Mkulima yeyote anayetilia maanani upepo hatapanda wakati upepo unapopuliza upande usiofaa" au 2) "Mkulima yeyote anayetilia maanani sana upepo hatapanda."

yeyote atazamaye mawingu yawezekana asivune

Maana zinazowezekana ni 1) "Mkulima yeyote anayetilia maanani mawingu hatavuna inapotaka kunyesha" au 2) "Mkulima yeyote anayetilia maanani sana mawingu hatavuna."

ambavyo mifupa ya mtoto ikuavyo

Maana zinazowezekana ni 1) "jinsi mtoto anavyokuwa" au 2) "jinsi mifupa ya mtoto inavyokua."

Ecclesiastes 11:6

kwa mikono yako

"endelea kufanya kazi"

jioni au asubuhi, au hii au ile

Misemo hii miwili inamaana moja na inasisitiza kuwa kazi ya mtu inaweza kufanikiwa, bila kujali ni muda gani aliifanya. "hata kama ni mbegu uliyoipanda asubuhi au mbegu uliyoipanda jioni."

nuru ni tamu

Hapa neno "nuru" inamaanisha kuweza kuona jua hivyo kuwa hai. "kuweza kuliona jua ni tamu" au "kuwa hai ni tamu."

kwa macho kuona jua

Msemo huu unamaana moja na usemi uliopita. "kwa mtu kuliona jua" au "kuwa hai."

aifurahie yote

Hapa neno "yote" inamaanisha miaka ambayo mtu yuko hai.

siku zijazo za giza

Hapa neno "giza" inamaanisha kifo. "atakuwa amekufa ziku ngapi."

kwa kuwa zitakuwa nyingi

Hapa "zitakuwa" inamaanisha "siku za giza." "kwa kuwa atakuwa amekufa siku nyingi zaidi ya zile atakavyokuwa hai au "kwa kuwa atakufa milele."

Kila kitu kijacho

Maana zinazowezekana ni 1) "Kila kitu kinachotokea baada ya kifo" au 2) "Kila kitu kitakachotokea baadaye."

Ecclesiastes 11:9

Furahia kijana, katika ujana wako, na moyo wako ufurahie siku za ujana wako

Misemo hii miwili inamaanisha kitu kimoja na imeunganishwa kwa ajili ya msisitizo.

moyo wako ufurahie

Hapa neno "moyo" inamaanisha hisia. "uwe na furaha"

Fuatilia yale mema ya moyo wako

Hapa neno "moyo" inaweza kumaanisha akili au hisia. "Fuatilia vitu vizuri unavyotamani" au "Fuatilia vitu vyema ulivyokusudia kufuatilia"

chochote kilicho mbele ya macho yako

"Chochote unachoona na kutamani" au "chochote unachoona kinafaa"

Mungu atakuleta hukumuni kwa ajili ya vitu hivi vyote

"Mungu atakuwajibisha kwa matendo yako yote"

Ondoa hasira kutoka moyoni mwako

"Kataa kuwa na hasira"

Ecclesiastes 12

Ecclesiastes 12:1

mkumbuke

"kumbuka"

Mimi sina furaha katika hizo

Hapa neno "hizo" linamaanisha "miaka."

Ecclesiastes 12:3

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaelezea nyumba ambayo matendo mbali mbali yanakoma. Hii inaonekana kuwa sitiari ya mwili wa binadamu unapozeeka.

wanawake wanao saga kukoma, kwa sababu ni wachache

"wanawake wanaosaga nafaka wanaacha kusaga nafaka kwa sababu ni wachache"

Ecclesiastes 12:4

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaendeleza sitiari yake.

milango imefungwa katika mtaa

"watu walifunga milango iliyoelekea katika mtaa"

wakati wanaume watasitushwa kwa mlio wa ndege

"wakati sauti ya ndege itakapowashtua"

Ecclesiastes 12:5

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaendeleza sitiari yake.

wakati ambapo hamu za asili zitakaposhindwa

"wakati ambapo watu hawatamani tena kile walichokuwa wanatamani kwa asili"

wakati ambapo mlozi utachanua maua

mti wa "mlozi" ni mti unaochanua wakati wa baridi na maua meupe.

mtu aenda katika nyumba yake ya milele

inamaanisha kifo.

waombolezaji watelemka mitaani

Maana zinazowezekana ni 1) waombolezaji wanaenda katika mtaa kuhudhuria mazishi, au 2) kwamba waombolezaji wanaenda mtaani kwenye nyumba ya mtu anayekaribia kufa.

Ecclesiastes 12:6

Mkumbuke

"kumbuka"

kabla ya kamba ya fedha kukatwa ... au torori la maji kuvunjika kisimani

Mwandishi anafananisha kifo na vitu mbali mbali vilivyovunjika. Kifo kitavunja mwili ghafla kama watu wavunjavyo hivi vitu wakati wakivitumia.

kamba ya fedha kukatwa

"mtu anakata kamba ya fedha"

bakuli ya dhahabu kupasuka

"mtu anapasua bakuli la dhahabu"

gudulia kuvunjwa

"Mtu anavunja gudulia"

torori la maji kuvunjika

"mtu anavunja torori la maji"

mavumbi kurudia aridhini

Hapa neno "mavumbi" inamaanisha mwili wa binadamu uliooza.

Ecclesiastes 12:8

kila kitu ni mvuke upoteao

"kila kitu kinadumu muda mfupi tu, kama mvuke unapotea."

kutafakari na kupanga

"aliwaza sana kuhusu na kupanga" au "aliwaza sana na kuandika chini"

Ecclesiastes 12:10

Maneno ya watu wenye hekima ... yamefundishwa na mchungaji mmoja

Mwandishi anamfananisha mwalimu anayetumia maneno yake kuelekeza watu na mchungaji anayetumia vifaa vyake kuongoza kundi lake.

Maneno ya watu wenye hekima ni kama mchokoo

"Watu wenye hekima wanatutia moyo kutenda, kama fimbo iliyochongoka inavyo watia hamasa wanyama kusogea.

Kama misumari ilivyogongomewa kwa undani, ndivyo yalivyo maneno ya mabwana katika mkusanyiko wa mithali zao

"Kama vile unavyoweza kuutegemea msumari uliozamishwa chini, ndivyo unaweza kutegemea mithali zilizoandikwa na watu wenye hekima."

maneno ya mabwana katika mkusanyiko wa mithali zao

"maneno ya wale ambao ni mahiri katika mikusanyiko ya mithali"

yamefundishwa na mchungaji mmoja

"ambayo mchungaji mmoja anafundisha"

Ecclesiastes 12:12

utengezaji wa vitabu vingi, ambapo hakuna mwisho

"watu hawatakoma kutengeneza vitabu vingi"

huleta uchovu mwilini

"humchosha mtu"

Ecclesiastes 12:13

Mwisho wa jambo

"hitimisho la mwisho la jambo"

baada ya kila kitu kusikika

"baada ya kusikia kila kitu"

Song of Songs 1

Song of Songs 1:1

Maelezo ya Jumla

Sehemu ya Kwanza ya kitabu yaanza 1:2.

Wimbo wa Nyimbo

"Wimbo ulio Bora" au Nyimbo iliyo Nzuri Sana"

ambao ni wa Sulemani

"unao muhusu Sulemani" au "ambao aliutunga"

mafuta yako ya upako

"Mafuta unayo paka mwilini mwako"

yana manukato mazuri

"yanukia vizuri"

jina lako ni kama marashi yaeleayo

Mwanamke anagundua kuwa mpenzi wake ana sifa nzuri. "jina lako ni zuri kama harufu ya mafuta mtu aliyo mimina

Nichukuwe nawe

"Ni lete pamoja nawe." Neno "wewe" la husu mpenzi

tutakimbia

Neno "tu" la husu mwanamke na mpenzi wake

kuhusu wewe

"kwasababu yako"

acha ni shereheke

"acha ni shereheke"

Ni halisi kwa wanawake wengine kukupenda

"Wote wanao kupenda wako sahihi"

Song of Songs 1:5

Mimi ni mweusi lakini mzuri

"Ngozi yangu ni nyeusi, lakini bado ni mzuri"

mweusi kama hema za Kedari

Makabila ya kuhama hama ya Kedari yalitumia ngozi nyeusi ya mbuzi kujenga nyumba zao. Mwanamke analinganisha ngozi yake na hizi hema.

mzuri kama mapazia ya Sulemani

Ana fananisha ngozi yake na mapazia mazuri Sulemani aliyo tengeneza ama kwa jumba lake au kwa ajili ya Hekalu.

limeniunguza

"kuchomwa"

Wana wa mama yangu

"Kaka zangu wa kambo." Hawa kaka zake labda walikuwa na mama mmoja kama huyu mwanamke lakini sie baba mmoja.

mtunzi wa mashamba ya mizabibu

"mtu aliye tunza shamba la mizabibu"

lakini shamba langu la mizabibu sijatunza

Mwanamke ana jilinganisha na shamba la mizabibu. "lakini sijaweza kujitunza mwenyewe."

Song of Songs 1:7

unalisha mifugo yako

"kulisha mifugo yako"

unapumzisha mifugo yako

"wanapo lala mifugo yako"

Kwa nini niwe kama mtu anaye akangaika miongoni mwa mifugo ya marafiki zako?

"Niambie ili nisitange miongoni mwa mifugo ya rafiki zako ninapo kutafuta"

angaika

"anaye zunguka"

marafiki

"jamaa" au "wafanya kazi wenza"

Song of Songs 1:8

fuata nyayo za mifugo yangu

"fuatisha nyuma ya mifugo"

nyayo

alama za kwato za mifugo kwenye ardhi

ulishe watoto wako wa mbuzi

"lisha watoto wa mbuz zako" au "acha mifugo yako ile"

Song of Songs 1:9

Maelezo ya Jumla

Mpenzi wa mwanamke anaendelea kuzungumza

mpenzi wangu

"ninaye mpenda"

na farasi mzuri wakike miongoni mwa farasi wa magari ya Farao

Mpenzi ana mlinganisha mwanamke na farasi mzuri wa kike.

magari ya farasi ya Farao

"Farasi wa Farao wanao vuta magari"

yaliochanganywa na fedha

"na madoa ya fedha"

Song of Songs 1:12

amelala kitandani mwake

"amekaa mezani mwake"

yakasambaza arufu

"yakatoa harufu yake nzuri"

nardo

mafuta watu wanayo tumia kufanya ngozi yao safi na nyororo.

Mpenzi wangu ni kwangu kama

"Kwangu mimi, mpenzi wangu ni kama"

lala usiku katikati ya maziwa yangu

"analala katikati ya maziwa yangu usiku kucha." Wanawake wanaweka kiasi kidogo cha manemane ya gharama kifuani mwao kuwapa harufu nzuri.

mua ya hena

maua kutoka jangwa dogo la miti watu walio tumia kama marashi

Song of Songs 1:15

Ona

Neno "Ona" hapa la ongeza msisitizo kwa kinacho fuata.

macho yako ni kama ya hua

Hua ni ishara ya usafi, bila hatia, upole na upendo. "macho yako ni mapole na mazuri kama ya hua.

Song of Songs 1:16

Ona

Neno "Ona" hapa la ongeza msisitizo kwa kinacho fuata.

mtanashati

"muonekano mzuri" au "mzuri" au "pendeza"

Nguzo za nyumba yetu ni za matawi ya mierezi

Mwanamke anaeleza msitu kama ni nyumba yao. "Matawi ya mti wa mierezi ni kama nguzo za nyumba yetu.

nguzo

mbao kubwa zinazo saidia nyumba yote

na boriti zetu ni matawi ya miberoshi

"na matawi ya miberoshi ni kama boriti zetu

boriti

vipande vya mbao vinavyo shikilia dari la nyumba

Song of Songs 2

Song of Songs 2:1

Mimi ni ua katika tambarare

Mwanamke anajilinganisha na ua katika tambarare

Tambarale

Sehemu ya ardhi ambayo iko sawa, haina miti, na huota aina nyingi za majani na maua

Nyinyoro katika bande

Mwanamke anajilinganisha mwenyewe na nyinyoro katika bonde ni sawa na kujilinganisha mwenyewe na maua yaliyo katika tambarale

Nyinyoro

ua lenye harufu nzuri lililo na umbo kama tarumbeta

Bonde

Hii ina maana ya sehemu kubwa iliyo sawa katikati ya milima

kama nyinyoro ...mwananchi wangu

Mwanaume ana maanisha mwanamke huyo ni zaidi ya mzuri na wathamani kuliko wanawake wadogo wote, kama nyinyoro ni zaidi ya ua zuri na lenye thamani kuliko miiba yote ya porini iliyo lizunguka

Mpenzi wangu

Ona ilivyo tafsiriwa hii katika 1:9

Binti wa mwananchi wangu

"Wanawake wadogo wengine"

Song of Songs 2:3

Kama mti wa mpera ... kijana mdogo

Kama mti wa mpera ni zaidi ya faraja na furaha zaidi ya miti yote msituni kwa hiyo mpendwa wa mwanamke ni zaidi ya faraja na furaha zaidi ya wanaume wadogo wote

Mti wa mpera

Mti unaozaa matunda madogo ya njano ambayo ni matamu sana

Nina kaa chini ya kivuli chake kwa furaha sana

Mwanamke anapata furaha na faraja akiwa karibu na mpendwa wake

Na tunda lake ni tamu kwa ladha yangu

Mwanamke analinganisha starehe anayo ipata kwa mpendwa wake na tunda tamu

Ukumbi wa maakuli

Ni chumba kikubwa ambapo watu hula mlo mkubwa na kufurahia kutembeleana

Na bendera yake

"bendera" ni kipande kikubwa cha nguo ambacho watu hupeperushwa juu mbele ya jeshi ili kuongoza na kuwapa ujasiri wanaume wengine

Bendera yake juu yangu ilikuwa upendo

Mwanamke angeweza kuwa na wasiwasi wa kuingia ukumbi wa maakuli, lakini mapenzi ya mpendwa wake yalimuonesha njia na kumpa ujasiri wa kuingia. "lakini upendo wake uliniongoza nakunipa ujasiri kama bendera."

Song of Songs 2:5

Ni uishe

"Nirudishie uwezo wangu" au "Nipatie nguvu"

Keki za mizabibu

"kwa kunilisha mikate iliyo tengenezwa na mizabibu iliyonata pamoja kama chapati" au "'kwa kunipa keki za mizabibu"

Ni nuishe kwa mapera

"nifadhili kwa kunipa mapera" au "nisaidie kwa kunipa mapera"

Kwakuwa nimedhohofika na mapenzi

"kwasababu mapenzi yangu yana nguvu sana hadi najiskia dhaifu."

Mkono wa kushoto ... mkono wa kulia

"mkono wa kushoto ... mkono wa kulia"

Wanikumbatia

"kunishikilia"

Song of Songs 2:7

Mabinti wa Yerusalemu

"wanawake wadogo wa Yerusalemu"

Kwa swala na paa wa porini

Wanyama hawa wa porini wana aibu na uwoga, lakini waza uzoefu wa uhuru kabisa.

Swala

Wanyama wanafanana kabisa na hayala na wapo haraka, wembamba na wana aibu

Wa porini

"ambao wanaishi upande wa nchi"

Hatuta vuruga mapenzi yetu hadi yatakapoisha yenyewe

"hatuta jivuruga tukiwa katika mapenzi hadi yatakapo isha"

vuruga

"Ghasia" au "Usumbufu"

Song of Songs 2:8

Oh, huyu yuwaja

Neno "Oh" hapa linaongea msisistizo kwa kile kinachofuata.

Akiruka ruka juu ya milima,akiruka vilimani

"akiruka juu ya milima , akikimbia haraka juu ya vilima ." Mpenzi anakimbia haraka na mwenye neema kama swala, hata juu ya ardhi mbaya ya milima na vilima.

Kama swala au mtoto mdogo wa paa

Mwanamka anamlinganisha mpenzi wake na swala au paa mdogo kwasababu yupo haraka, mzuri, na mwenye neema kama wanyama hawa.

Swala

Ona jinsi ilivyotafsiriwa "swala" katika 8:2

Mtoto mdogo wa paa

"paa mdogo" au "mwana mdogo wa hayala"

Tazama, amesimama

Neno "tazama" hapa linaonesha kwamba mwanamke ameona kitu cha kuvutia.

Nyuma ya ukuta wetu

"upande mwengine wa ukata wetu." Mwanamke yupo kwenye nyumba na mpenzi wake yupo njee ya nyumba.

akishangaa kupitia dirishani

"anatazama kupitia madirisha"

akichungulia wavuni

"anashangaa kupitia wavuni"

wavu

vipande virefu vya mbao mtu alivyo viunga pamoja ili kutengeneza mfuniko wa dirisha au mwingilio tofauti

Song of Songs 2:10

Amka

"Nyanyuka juu"

mpenzi wangu

Ona jinsi ulivyo tafsiri 1:9

Angalia, baridi imepita

Neno "Angalia" hapa laongeza mkazo kwa linalo fuata.

mvua imeisha na kwenda

Katika Israeli, kunanyesha kipindi cha mvua tu.

Song of Songs 2:12

Maua yametokeza

"Waeza ona maua" au "Watu wanaeza ona maua."

juu ya nchi

"katika nchi yote hii"

wakati wa kupunguza matawi

"majira ya watu kupunguza matawi"

na kuimba kwa ndege

" na ndege kuimba"

sauti za hua zimesikika

"waeza sikia hua wakilia" au "watu waeza sikia sauti za hua"

mizabibu imestawi

"mizabibu imetoa maua" au "mizabibu ina maua"

yatoa

Neno "ya" linahusu kustawi kwa mizabibu.

marashi

"arufu nzuri"

Song of Songs 2:14

Maelezo ya jumla:

Mpenzi wa mwanamke anaongea.

Hua wangu

Mpenzi wa mwanamke anamlinganisha mwanamke na hua kwasababu ana sura nzuri na sauti nzuri kama ya hua na kwasababu alikuwa awe naye katika sehemu ya mbali na watu kama hua anavyo ishi eneo la mbali na watu.

katika miamba ya mawe

"sehemu ya kujificha ya miamba." Miamba ni mipasuko mikubwa ya mawa ya milimani.

katika miamba ya siri ya mipasuko ya milima

"katika sehemu za siri za mporomoko wa mlima." Maneno haya yanaeleza sehemu ambayo mpenzi anataka kuona sura ya mwanamke

sura yako

"muonekano wako" au "ufumo wako" au "uonekanavyo"

Song of Songs 2:15

mbweha

Hili ya weza kutafsiriwa kama "mbwa mwitu." Hawa wanyama wanaonekana kama mbwa wadogo na mara nyingi walitumika kwenye mashahiri ya mapenzi kuwakilisha wanaume vijana wenye shauku wanaoweza kumpumbaza binti.

yetu

Neno "yetu" la weza kumaanisha 1) mwanamke na mpenzi wake au 2) mwanamke na familia yake nzima.

mbweha wadogo

Mbweha wanazaa watoto wao majira ya masika mizabibu inapo chipua.

wanao haribu

"wanao vuruga" au "wanao angamiza." Mbweha na mbwa mitu wanaharibu mashamba ya mizabibu kwa kuchimba mashimo na kula mizabibu na mizaituni. Hii pia yaweza wakilisha wanaume vijana wanao haribu mabinti.

limestawi.

Hii yaweza wakilisha mwanawake mdogo aliye tayari kwa ndoa na kuzaa watoto. Ona jinsi ulivyo tafsiri hii 2:12

Song of Songs 2:16

Mpenzi wangu ni wangu

"Mpenzi wangu ni sehemu yangu"

na mimi ni wake

"na mimi ni sehemu yake"

anakula

"ujishibisha" au "ula majani." Mwanamke anamlinganisha mpenzi wake na mnyama anaye kula mimea miongoni mwa nyinyoro, kama paa au ayala mdogo.

vivuli kutoweka

Mwanamke anaeleza vivuli kama vile vinakimbia wanga wa jua.

kama ayala au mtoto mdogo wa paa

Ona jinsi ulivyo tafsiri 2:8

ayala

aina ya mafano wa swala wenye pembe zilizo pinda

paa

swala wa kiume

Song of Songs 3

Song of Songs 3:1

nilikuwa na shauku ya yeye ni mpendaye; nilimtafuta

Hii imerudiwa kwa mkazo.

nilimtafuta, lakini sikumpata

"nilikuwa nataka kuwa naye" au "nilikuwa na shauku naye"

nilikuwa na shauku ya yeye ni mpendaye

Ona jinsi ulivyo tafsiri "yeye nafsi yangu impendaye" 1:7

kwenda kupitia mji

"kutembea mjini"

kupitia mitaa na sokoni

Neno "sokoni" la ashiria eneo la katikati ya mji ambapo mitaa na barabara uja pamoja. Ni sehemu ambapo watu uuza vitu, eneo la bihashara, na sehemu watu wanakuja kunzungumza pamoja.

Nilimtafuta

"kumtafuta"

Song of Songs 3:3

Walinzi

watu wenye wajibu wa kulinda mji usiku kuwa weka watu salama

walipo kuwa doria katika mji

"walio kuwa wakipita kwenye mji" au "walio kuwa wanatembea mjini

kitandani

"chumba walichokuwa wanalala"

yeye aliyenichukua mimba

"yeye aliye beba mimba na mimi" au "yeye aliye ni beba tumboni mwake" Hii ina maana ya mama yake.

Song of Songs 3:5

Ninataka muape ... yatakapo isha

Ona jinsi ulivyo tafsiri 2:7

Song of Songs 3:6

Maelezo ya Jumla

Hapa ni mwanzo wa Sehemu ya Tatu ya kitabu

Nini hiyo inayo toka nyikani

Kundi la watu wanao safiri kutoka nyikani kwenda Yerusalemu. Kwasababu nyikani iko chini ya bonde la Yordani na Yerusalemu iko juu ya milima, watu lazima waende juu kufikia Yerusalemu.

kama nguzo za moshi

Kwasababu watu walitimua vumbi sana walipo kuwa wakisafiri, vumbi lilionekana kama moshi kwa mbali.

umefukizwa manemane na ubani

"harufu nzuri ya moshi wa manemane na uvumba umeizunguka."

pamoja na unga wote wa manukato unao uzwa na wafanya biashara

"na harafu nzuri ya moshi wote unga wafanya bihashara wanauza."

unga

udogo safi unao patikana kwa kusaga kitu kigumu

Angalia

Hili neno hapa linaonyesha kuwa mnenaji sasa amegundua jibu kwa swali la mstari wa 6.

nikitanda

Hii ya husu kitanda chenye shuka linalo weza kubwa sehemu moja kwenda nyingine.

mashujaa sitini wamekizunguka, wanajeshi elfu sitini wa Israeli

Hii mistari miwili ya husu watu hao hao sitini. Mstari wa pili wa fafanua kuwa "mashujaa" ni "wanajeshi wa Israeli."

mashujaa

wanaume wanao pigana

Song of Songs 3:8

wa vita

"katika pambano"

akijizatiti na

"ilikuji linda dhidi ya" au "kuweza kupigana na"

maasi ya usiku

Hii ya husu hatari yeyote inayo weza kuja giza la usiku, kama majambazi.

kiti cha kifalme

kiti chenye miti mirefu watu wanacho tumia kubeba watu muhimu

Song of Songs 3:10

Nguzo zake

Neno "zake" la husu kiti cha Mfalme Sulemani.

Nguzo

Neno "nguzo" hapa la husu vipande vya mbao vinvyo shikilia kitambaa cha hema kwenye kiti chake.

Ndani mwake

"Ndani yake kulikuwa"

kulipambwa na upendo

"kulifanywa pazuri kwa upendo" au "kulishonewa upendo." Hii ya hashiria kwamba wanawake walifanya kiti cha mfalme kizuri kwa namna ya kipekee kuonyesha upendo wao kwa Sulemani.

na mtazame mfalme Sulemani

"muone mfalme Sulemani." Neno "tazama" la husu kumuangalia mtu au kitu kwa muda mrefu, mara nyingi kwa hisia kali.

akivikwa taji

"amevaa taji"

Song of Songs 4

Song of Songs 4:1

O, wewe ni mzuri ... Macho yako ni ya hua

Ona jinsi ulivyo tafsiri 1:15

Nywele zako ... Mlima Gileadi

Mbuzi mara nyingi ni weusi kwa rangi na wanapo tembea milimani nywele zao zinaonekana kama mawimbi ya nywele za mwanamke.

Song of Songs 4:2

Meno yako ni kama kondoo walio nyolewa

Baada ya kondoo kunyolewa, wameoshwa na ngozi yao yaonekana nyeupe sana. Haya maneno yalinganisha weupe wa meno ya mwanamke na mng'ao mweupe wa manyoya ya kondoo baada ya manyoya yao kunyolewa.

wakitoka sehemu ya kuoshwa

Hii ina maana kondoo wanatoka kwenye maji. "wakitoka kwenye maji baada ya watu kuwaosha"

Kila mmoja ana pacha

Kwa kawaida kondoo uza wana kondoo wawili kwa wakati mmoja. Hawa wana kondoo huwa wamefanana. Kila meno ya mwanamke yana jino linalo fanana upende wa pili wa mdomo wake. Hivyo ni kama kila jino lina pacha kama wana kondoo.

hamna ata mmoja miongoni mwao aliyefiwa.

Hakuna meno yao yaliyo poteza jino lingine linalo fanana upande wa pili. Mwanamke hajapoteza meno yake.

aliyefiwa

Kupoteza mpendwa aliye kufa.

Song of Songs 4:3

Maelezo ya Jumla

Mpenzi anaendelea kumsifu mwanamke.

kama uzi mwekendu

Haya maneno yanalinganisha rangi midomo ya mwanamke na uzi mwekundu.

wapendeza

"ni mzuri"

kama majani ya komamanga

Makomamanga yanateleza, ya duara, na yana rangi nyekundu.

nyuma ya kitambaa chako

Ona jinsi ulivyo tafsiri 4:1

Song of Songs 4:4

Maelezo ya Jumla

Mpenzi anaendelea kumsifu mwanamke.

Shingo yako ni kama

"shingo yako ni ndefu na nzuri kama"

wa Daudi

"mbao Daudi alijenga"

umejengwa kwa mistari ya mawe

Wanawake walikuwa na mikufu iliyo funika shingo zao kwa mistari ya mapambo. Mpenzi analinganisha hii mistari ya mapambo na mistari mistari ya mawe kwenye mnara.

na ngao elfu moja

Mpenzi analinganisha mapambo ya mkufu wa mwanamke na ngao zinazo ni'ng'nia kwenye mnara.

ngao elfu moja

"ngao 1,000."

ngao zote za wanajeshi

"ngao zote za mashujaa hodari"

kama swala wawili, mapacha wa ayala

Maziwa ya mwanamke ni mazuri, yamelingana na mepesi kama watoto wa wili wa swala aya wa ayala.

mapacha

watoto wa mama aliye zaa watoto wawili kwa wakati mmoja

ayala

Ona jinsi ulivyo tafsiri "ayala" 2:7

wakila miongoni mwa nyinyoro

"kula mimea miongoni mwa nyinyoro." Mapacha wazuri wawili na mtoto ayala ni wazuri zaidi wakati nyinyoro imewazungukaa.

Song of Songs 4:6

Maelezo ya Jumla

Mpenzi anaendelea kumsifu mwanamke.

Hadi jioni ifike na vivuli viondoke

Ona jinsi ulivyo tafsiri mstari 2:16 ambapo neno ni moja na hili.

nitaenda kwenye mlima wa manemane na vilima vya ubani

Mpenzi anaelezea matamanio yake ya kufurahia maziwa ya mwanamke kwa kulinganisha na milima au vilima anayo i penda. Maziwa yake ni duara na yametokeza kama milima au vilima. Yananukia vizuri kama manemane na uvumba.

nitaenda kwenye mlima ... vilima vya ubani

Hii mistari inarudia wazo kwa utofauti kidogo wa kukazia mvuto wa maziwa ya mpenzi.

mlima wa manemane

"mlima ulitengenezwa kwa manemane" au "mlima uliyo na manemane"

Wewe ni mzuri kwa kila namna

"Kila sehemu yako ni nzuri" au "Wewe wote ni mzuri"

mpenzi wangu

Ona jinsi ulivyo tafsiri 1:9

hakuna lawama ndani yako

"Hauna lawama"

Song of Songs 4:8

Maelezo ya Jumla

Mpenzi anaendelea kuongea na mwanamke.

Njoo nami ... shimoni mwa simba

Mpenzi anataka bibi arusi wake aje nae kutoka sehemu ya hatari. Hii ni fumbo na wala wapenzi hawapo kwenye hii milima au shimoni.

kutoka Lebanoni

"mbali kutoka Lebanoni"

Amana

jina la mlima karibu na Damsko

Seneri

jina la mlima karibu na Amana na Herimoni. Watu baadhi wanadhani hii ya husu mlima mmoja na Hermoni.

shimoni

Sehemu simba na chuwi wanaishi, kama mapango au mashimo kwenye ardhi

Song of Songs 4:9

Maelezo ya jumla

Mpenzi anaendelea kuongea na mwanamke.

Umeuiba moyo wangu

Anasema mapenzi yake na upendo wake ni wa mwanamke. "umenasa upendo wangu"

dada yangu

Mwanamke ana pendwa sana na mpenzi kama dada yake mwenyewe. Sio kaka na dada kihalisia.

kwa mtazamo mmoja tu wako kwangu, kwa mkufu mmoja wa shingo yako

Macho yote ya mwanamke na mikufu yake ina mvutia mpenzi kwake.

Song of Songs 4:10

Maelezo ya Jumla

Mpenzi anaendelea kumsifu na mwanamke.

Jinisi gani upendo wako ulivyo mzuri

"Upendo wako ni wa ajabu"

dada yangu, bibi arusi wangu

Ona jinsi ulivyo tafsiri 4:9

Jinsi gani zaidi upendo wako ulivyo bora kuliko mvinyo

Hii mistari inarudia wazo moja kwa maneno tofauti kwa kukazia.

Jinsi gani zaidi upendo wako ulivyo bora kuliko mvinyo

"Upendo wako ni bora kuliko mvinyo." Ona jinsi ulivyo tafsiri 1:1

arufu ya marashi yako kuliko manukato yeyote

"harufu ya mafuta yako ni bora kuliko harufu ya manukato yeyote."

marashi ... manukato

Ona jinsi ulivyo tafsiri haya maneno 1:1

Midomo yako ... chini ya ulimi wako

Hii mistari inarudia wazo moja kwa maneno tofauti kwa kukazia.

Midomo yako, bibi arusi wangu, yatiririka asali

Mpenzi anadhani mabusu ya mwanamke ni matamu kama asali; au, kwasababu maneno anayozungumza ni matamu kama asali.

asali na maziwa vichini ya ulimi wako

Mpenzi anadhani mabusu ya mwanamke ni matamu kama asali; au, kwasababu maneno anayozungumza ni matamu kama asali.

arufu ya mavazi yako ni kama marashi ya Lebanoni

"harafu ya nguo zako ni kama harufu ya Lebanoni." Miti mingi ya mierezi yaota Lebanoni. Miti ya mierezi yanukia vizuri, hivyo Lebanoni ingenukia vizuri.

Song of Songs 4:12

Maelezo ya Jumla

Mpenzi anaendelea kumsifu mwanamke.

Dada yangu, bibi arusi wangu

Ona jinsi ulivyo tafsiri 4:9

ni bustani ilio fungwa

Mpenzi anamlinganisha mwanamke na bustani iliyo fungwa kwasababu yeye ni wake tu na anaweza mfurahia. Anaweza pia kusema kuwa yeye bado ni bikra ambaye bado hajamfurahia.

chemchemi iliyo fungwa kwa muhuri

Mpenzi anamlinganisha mwanamke na chemchemi iliyo fungwa kwa muhuri kwasababu zile zile alizo mlinganisha na bustani iliyo fungwa.

Matawi yako ... aina tofauti za manukato

Mpenzi anamuelezea jinsi mwanamke alivyo mzuri kwa kumfananisha kama bustani iliyo jaa vitu vizuri.

kichaka

sehemu miti mingi inapo ota pamoja

yenye matunda tofauti

"matunda mbali yaliyo bora"

hina

Ona jinsi ulivyo tafsiri 1:12

Nardo

Ona jinsi ulivyo tafsiri 1:12

Zafarani

kiungo kinacho toka kwenye sehemu iliyo kauka kutoka kwenye uzi wa chano katikati ya ua.

mchai

Hili ni jani lenye harufu nzuri ambalo watu wanatumia kutengeneza mafuta ya upako.

mdalasini

kiungo kilicho tengenezwa na ganda la mti ambalo watu utumia kupika

manemane

Ona jinsi ulivyo tafsiri 1:12

aloes

aina kubwa ya mmea wenye harufu nzuri sana

aina zote za uvumba

"uvumba bora"

Song of Songs 4:15

Maelezo ya Jumla

Mpenzi anaendelea kumsifu mwanamke.

Wewe ni bustani ya chemchemi

"Wewe ni chemchemi katika bustani." Mpenzi ana elezea jinsi alivyo mzuri kwa kumfananisha na maji.

maji safi

maji safi ya kunywa

mifereji inayo shuka kutoka Lebanoni

Kwasababu Lebanoni ilikuwa na milima iliyo funikwa kwa miti, mifereji kutoka Lebanoni ilikuwa misafi na ya baridi.

Amka ... manukato yake yatoe marashi

Mwanamke anazungumza na upepo wa kaskazini na wa kusini kama ni watu.

Amka

"Anza kwenda"

vuma katika bustani yangu

Mwanamke ana utaja mwili wake kwa kuuongelea kama bsutani.

ili manukato yake yatoe marashi

"itume harufu yake nzuri"

Mpenzi wangu na ... matunda ya chaguo

Mwanamke anamkaribisha mpenzi wake kumfurahia kama mkewe.

matunda ya chaguo

"matunda mazuri"

Song of Songs 5

Song of Songs 5:1

Nimekuja

Ni dhahiri kuwa mpenzi wa mwanamke anazungumza.

nimekuja katika bustani yangu

Mwanamme anaelezea mwanamke kama bustani. Usiku wa arusi, mwanamme anaweza kumfurahia mwanamke. Anaelezea hili kama kuja katika bustani yake.

dada yangu

Mwanamme anamuita mwanamke dada kwasababu mpenda sana kama angempenda dada yake. "yeye ni mpendaye"

Nimekusanya udi wangu ... na maziwa yangu

Mwanamme anatumia haya maumbo kutoka kwenye bustani kuhashiria kwamba ameweza kufurahia sehemu nyingi za mwanamke.

manukato

mimea yenye harufu nzuri au ladha

Song of Songs 5:2

Maelezo ya Jumla

Hapa ni mwanzo wa Sehemu ya Nne ya kitabu

Maelezo ya Jumla

Mwanamke anatumia tafsida kueleza ndoto yake ili kwamba iweze kutafsiriwa kwa njia mbili tofauti: 1) mwanamke anaeleza ndoto kuhusu usiku mpenzi wake alipo kuja kumtembelea nyumbani mwake; na 2) mwanamke anaeleza ndoto kuhusu kuanza kulala na mpenzi wake.

lakini moyo wangu ulikuwa umeamka

"lakini moyo wangu ulikuwa umeamka"

Nifungulie

Hii ya husu kufungua mlango lakini yaweza tafsiriwa kama ombi la kimapenzi. "Fungua mlango kwa ajili yangu" au "Jifungue kwangu"

dada yangu

Maneno ya mahaba. Ona jinsi ulivyo tafsiri 4:9

mpenzi wangu

Ona jinsi ulivyo tafsiri 1:9

hua wangu

Ona Jinsi ulivyo tafsiri 2:14

usiye na doa

"mkamilifu wangu" au "mwaminifu wangu" au "usiye na hatia wangu"

unyevu

matone ya maji au ukungu unaoa kuwa wakati wa baridi ya usiku hali ya hewa inaposhuka

nywele zangu na unyevu wa usiku

hewa nyevu ya usiku ya fanya nywele za mwanamme kulowa kwasababu kasimama nje.

kichwa changu kimelowa na matone, nywele zangu na unyevu wa usiku

Hii mistari miwili ina maanisha kitu kimoja.

Song of Songs 5:3

joho

nguo nyembamba watu waliyo vaa kwenye ngozi yao

lazima nilivae tena?

"sitaki kuvalishwa tena"

Nimeosha miguu yangu

Tafsiri zinazo wezekana ni 1) mwanamke aliosha miguu yake ili aweze kwenda kitandani au 2) Neno "miguu" wakati mwengine la tumika kama tafsida kueleza sehemu za siri za mwanamke. "nimejiosha"

Mpenzi wangu anaeka mkono wake kwenye kitasa

Tafsiri zinazo wezekana ni 1) mpenzi anafikia nyumbani kwa kupitia kitobo kwenye mlangao ili kufungua mlango au 2) huu ni mwanzo wa tendo la mapenzi. Katika huu muktadha, "mkono" waelezewa kama tafsida ya sehemu za siri za mwanamme.

Mpenzi wangu

Ona jinsi ulivyo tafsiri 1:12

kitasa

"kufuli"

Song of Songs 5:5

Nimeamka kumfungulia mlango mpenzi wangu

Tafsiri zinazo wezekana ni 1) mwanamke aliinuka kutoka kitandani kuweza kumuingiza mpenzi wake ndani ya nyumba au 2) "Nimejianda kuweza kujifungua kimapenzi kwa mpenzi wangu."

mikono yangu ... vidole vyangu

Maneno "mikono" na "vidole" yaweza kumaanisha viungo vya siri vya mwanamke.

unyevu wa udi

"kwa udi wa maji"

Song of Songs 5:6

Maelezo ya Jumla

Mwanamke anaendelea kueleza ndoto yake.

Nimemfungulia mlango mpenzi wangu

"Nimejifungua kwa mpenzi wangu."

mpenzi wangu

Ona jinsi ulivyo tafsiri 1:12

Moyo wangu ukadidimia; nikakosa tumaini

"Moyo wangu ukaondoka." Alipo zungumza, nilihisi kama nimekufa"

Song of Songs 5:7

Walinz

wao wanao kesha na kulinda mji usiku

walinipata mimi

Neno "mimi" la muhusu mwanamke.

askari katika ukuta

wanaume wanao linda kuta"

nguo yangu ya juu

nguo ya nje ambayo watu wanavaa juu ya nguo yao ingine sehemu ya mabegani wanapo enda sehemu ya hadhara.

Song of Songs 5:8

Ninataka uhaidi, mabinti wa Yerusalemu

Ona jinsi ulivyo tafsiri "Ninataka uhaidi, mabinti wa Yerusalemu," 2:7

ninaumwa sababu ya upendo wangu kwake

Upendo wake una nguvu hadi anaumwa.

Song of Songs 5:9

wewe uliye mzuri miongoni mwa wanawake

Ona jinsi ulivyo tafsiri "mzuri miongoni mwa wanawake" 1:8

Kwanini mpenzi wako bora

"Nini ya mfanya mpenzi wako bora"

hadi utuulize tuweke nadhiri kama hii

"na ana kusababisha utufanye tu chukuwe nadhiri kama hii"

nadhiri kama hii

Ona hiyo nadhiri 5:8

Song of Songs 5:10

amenawiri na ana ng'aa

Yaelezwa kuwa mwanamke ana eleza ngozi ya mpenzi wake.

amenawiri

"ana afya tele" au "ni msafi." Mpenzi ana ngozi ambayo haina shida.

kati ya wanaume elfu kumi

"bora ya 10,000" "bora kuliko yeyote" au "hakuna aliye kama yeye"

Kichwa chake ni dhahabu safi

Kichwa cha mpenzi kina thamani kwa mwanamke kama dhahabu safi.

kunguru

ndege mwenye manyoya meusi sana

Song of Songs 5:12

Maelezo ya Jumla

Mwanamke anaendelea kumuelezea mpenzi wake.

Macho yake ni kama ya hua

Ona jinsi ulivyo tafsiri "macho yako ni kama ya hua" 1:15

pembezoni ya vijito vya maji

Mwanamke anaweza kuwa anatumia hili umbo kusema kwamba macho ya mpenzi wake ya unyevu kama mifereji ya maji.

yameoshwa na maziwa

"yamejiosha yenyewe katika maziwa." Hua wanawakilisha watoto wa mpenzi. Haya yamezungukwa na macho yake yote, ambayo ni meupe kama maziwa.

yameundwa kama mikufu

Macho yake ni mazuri hadi yanaonekana kama madini ambayo sonara ameyaweka pamoja.

Song of Songs 5:13

Maelezo ya Jumla

Mwanamke anaendelea kumuelezea mpenzi wake.

Mashavu yake ... arufu ya marashi

Hii ya fafanua kuwa mashavu yake ni kama vitanda vya manukato kwasababu vyote vinatoa harufu nzuri.

vitanda vya manukato

bustani au sehemu ya bustani watu wanapo otesha manukato

vinavyotoa arufu ya marashi

"vinavyotoa harufu nzuri"

Midomo yake ni nyinyoro

Mwanamke inawezekana ana linganisha midomo yake na nyinyoro kwasababu ni mizuri na inanukia vizuri.

tiririka udi

"inayo tiririka na udi uliyo bora." Midomo yake ni minyevu na inanukia vizuri kama udi.

nyinyoro

Ona jinsi ulivyo tafsiri 2:16

Song of Songs 5:14

Maelezo ya Jumla

Mwanamke anaendelea kumuelezea mpenzi wake.

Mikono yake ni ya mianzi ya dhahabu

Mwanamke anatumia hili umbo kusema kwamba mikono yake ni mizuri na ya thamani.

tumbo lake ni pembe lililo funikwa yakuti samawi

Mwanamke anatumia hili umbo kusema kwamba tumbo lake ni zuri na ya thamani.

yakuti samawi

Yakuti samawi ni ya jiwe safi na la thamani. Hili aina ya yakuti samawi lina njano au rangi ya dhahabu.

Song of Songs 5:15

Maelezo ya Jumla

Mwanamke anaendelea kumuelezea mpenzi wake.

Miguu yake ni nguzo za marimari

Miguu yake ina nguvu na mizuri kama marimari ya nguzo

Marimari

jiwe lenye imara lenye rangi tofauti na watu wana lisugua kulifanya nyororo

iliyo ekwa juu ya dhahabu safi

Miguu yake ina thamani kama chini ya dhahabu safi inayo wezezesha nguzo za marimari.

muonekano wake ni kama Lebanoni

Lebanoni ili kuwa eneo zuri lenye milima mingi na miti.

mizuri kama mierezi

"yenye kutamanika kama mierezi" au "vyema kama mierezi"

Song of Songs 5:16

Maelezo ya Jumla

Mwanamke anaendelea kumuelezea mpenzi wake.

Mdomo wake ni mtamu

Mwanamke anatumia hili umbo kuelezea utamu wa busu la mpenzi wake au maneno matamu anayo sema.

ni mzuri sana

"kila sehemu yake ni nzuri" au "yeye ni mzuri"

Huyu ni mpenzi wangu, na huyu ni rafiki yangu

Neno "Huyu" la muelezea mtu mwanamke aliye maliza kumuongelea. Waweza pia tafsiri haya maneno kama "Yule ni mpenzi wangu, na hivi ndivyo rafiki yangu alivyo."

mabinti wa Yerusalemu

Ona jinsi ulivyo tafsiri 1:5

Song of Songs 6

Song of Songs 6:1

Kwa njia gani mpenzi wako ameenda

"mpenzi wako ameelekea wapi"

ulio mzuri miongoni mwa wanawake

Ona jinsi ulivyo tafsiri 1:8

ilitumtafute nawe?

"Tuambie, ilitumtafute kwa pamoja."

Song of Songs 6:2

Mpenzi wangu ameenda katika bustani yake

Ona ufafanuzi wa umbo hili 5:1

vitanda vya manukato

Ona jinsi ulivyo tafsiri " vitanda vya manukato" katika 5:13. Mpenzi amekuja kufurahia mvuto wa mwili wa mwanamke ambao ni mzuri kama manukato.

kula katika bustani na kukusanya nyinyoro

Mwanamke anatumia haya maumbo kuhashiria kwamba mpenzi wake ana mfurahia yeye.

kula

Ona jinsi ulivyo tafsiri "ana kula" 2:16

kukusanya nyinyoro

"kuokota nyinyoro"

nyinyoro

Ona jinsi ulivyo tafsiri 2:16

Mimi ni wa mpenzi wangu, na mpenzi wangu ni wangu

Ona jinsi ulivyo tafsiri "Mpenzi wangu ni wangu na mimi ni wake" 2:16

na kula katika nyinyoro kwa raha

Ona jinsi ulivyo tafsiri 2:16

Song of Songs 6:4

Maelezo ya Jumla

Hapa ni mwanzo wa Sehemu ya Tano cha kitabu

ni mzuri kama Tirza, mpenzi wangu, wapendeza kama Yerusalemu

Mpenzi ana fananisha uzuri wa mwanamke na mvuto wake kwa miji mizuri na ya kuvutia.

wapendeza

Ona jinsi ulivyo tafsiri 1:5

waamasisha kama jeshi lenye bendera mbele

waamasisha kama jeshi lenye bendera mbele Uzuri wa mwanamke ni una nguvu hadi unamfanya mpenzi ahisi hana msaada, kama jeshi lilikuwa linamfuata.

Song of Songs 6:5

Maelezo ya Jumla

Mwanamke anaendelea kumsifu mwanamke.

yana nizidi ukali

"kuniogopesha." Macho ya mwanamke ni mazuri hadi yana mfanya mpenzi kuhisi kuzidiwa na kuogopa kwasababu haweza zuia nguvu.

Nywele zako ... kutoka miteremko ya Mlima Gileadi

Ona jinsi ulivyo tafsiri "Nywele zako ... kutoka Mlima Gileadi" 4:1

Song of Songs 6:6

Maelezo ya Jumla

Mpenzi anaendelea kumsifu mwanamke.

Mashavu yako ni kama majani ya komamanga nyuma ya kitambaa chako cha uso

Ona jinsi ulivyo tafsiri 4:3

Song of Songs 6:8

Kuna malikia sitini, masuria themanini

Kuna malikia 60, masuria 80."

wanawake wadogo bila idadi

Maneno, "bila idadi" yamaanisha hakuna anaweza kuwahesabu. "maelfu ya wanawake wadogo"

Hua wangu, asiye na doa wangu

Ona jinsi ulivyo tafsiri "Hua wangu, asiye na doa wangu" 5:2

ni yeye pekee

"ni wa pekee" au "ni mmoja wa wachache." Mpenzi ana mtofautisha mwanamke na wanawake wengine. Japo kuwa kuna wanawake wema wengi, mwanamke ana simamawa kipekee miongoni mwa wote.

ni binti muhimu wa mama yake

"kwa mama yake ni binti maalumu" au "yeye ni binti wa mama yake ambaye ni wa kipekee"

mwanamke aliye mzaa

"mwanamke aliye mzaa." Haya maneno ya muongelea mama yake.

na kumuita mbarikiwa

"na kukiri kuwa mambo yamemuendea vizuri" au "kusema kuwa yeye alikuwa na bahati"

Song of Songs 6:10

Maelezo ya Jumla

Yale malikia na masuri walisema kuhusu mwanamke. Ingawa, tafsiri zingine zinaona kuwa mpenzi wa mwanamke anaongea katika huu mstari pia.

Ni nani huyo anaye jitokeza kama kukicha

Wanatumia hili swali kusema kuwa wanadhani mwanamke ni wa ajabu.

anaye jitokeza kama kukicha

Mpenzi anatumia hili umbo kusema kuwa mwanamke ni mzuri na wa utukufu kama kunavyo pamba zuka na kung'aa.

waamasisha kama jeshi lenye bendera mbele

waamasisha kama jeshi lenye bendera mbele Uzuri wa mwanamke ni una nguvu hadi unawafanya wanawake wahisi hawana msaada, kama jeshi lilikuwa linamfuata. Ona jinsi ulivyo tafsiri 6:4

Song of Songs 6:11

Maelezo ya Jumla

Mpenzi anaendelea kuongea mwenyewe.

milozi

Ona jinsi ulivyo tafsiri 4:12

mimea midogo

"mimea michanga" au "matawi mapya"

imestawi

"imefungua maua yake"

Nilikuwa nina furaha nikahisi kama nimepakia gari ya farasi la mtoto wa mfalme

Mpenzi anatumia umbo hili ili kuonyesha jinsi alivyo na furaha.

Song of Songs 6:13

Geuka nyuma, geuka nyuma

Hii imerudiwa kwa mkazo.

kukushangaa

kuangalia kitu kwa umakini kwa muda

kana kwamba nina cheza katika ya mistari miwili ya wachezaji

Ingekuwa kitu kizuri kuona mwanamke akicheza na wachezaji wengine.

Song of Songs 7

Song of Songs 7:1

Jinsi gani miguu yako ilivyo yaonekana mizuri kwenye viatu

Ina hashiriwa kwa muendelezo kutoka 6:13 kuwa mpenzi wa mwanamke ana muelezea akiwa anacheza. "Miguuu yako ni mizuri sana ndani ya viatu vyako."

binti wa mfalme

Japo mwanamke hakuzaliwa katika familia ya kifalme, jinsi anavyo onekana na kutenda ana sababisha kuonekana kama binti wa mfalme. "una tabia njema" au "wewe uliye mrembo"

Mapaja yako ni kama mikufu

Umbo la mapaja ya mwanamke ni kama madini ya thamani ambaye mjuzi wa kutengeneza ame ya chonga kikamilifu.

Mapaja yako

Neno "mapaja" ya lina husu sehemu ya mwili wa mwanamke uliyo juu ya magoti.

Song of Songs 7:2

Maelezo ya Jumla

Mpenzi wa mwanamke anaendelea kumuelezea yeye anaye mpenda

Kitovu chako ni kama duara la bakuli

Kitovu cha mwanamke kina umbo zuri kama kibakuli.

Kitovu

Sehemu illiyo ingia ndani katika tumbo, ambayo ni kovu lililo baki ambalo lilimuunganisha mtoto na mama yake

kamwe kisikose mchanganyiko wa mvinyo

Watu walitumia mitungi mikubwa kuchanganya maji na mvinyo au theluji kwa ajili ya sherehe. Watu walifurahia ladha ya mvinyo kwenye sherehe.

Tumbo lako ni kama ngano iliyo umuka

Watu walidhani kuwa rangi ya ngano ni nzuri sana ya mwili na kwamba ngano iliyo umuka ya duara ni nzuri. "Tumbo lako lina rangi nzuri na liladuara kama ngano iliyo umuka."

ngano iliyo umuka

Hii ni ngano iliyo kusanywa baada ya watu kuipeta na kuisaga.

kuzungushiwa nyinyoro

Maua mazuri yanafanya ngano iliyo petwa na kukusanywa kuonekana nzuri.

nyinyoro

aina ya maua makubwa

Song of Songs 7:3

Maelezo ya Jumla

Mpenzi wa mwanamke anaendelea kuelezea yeye anaye mpenda.

Maziwa yako mawili ni kama watoto wawili wa ayala, mapacha wa ayala

Ona jinsi ulivyo tafsiri: 4:4

Shingo yako ni kama mnara wa pembe

Mpenzi analinganisha shingo yake na mnara uliyo tengenezwa kwa madini ya mapembe.

macho yako ni kama maziwa ya Heshiboni

"macho yako ni meupe na yana ng'aa kama mabwawa ya maji ya Heshiboni."

Heshiboni

jina la mji wa mashariki wa mto wa Yordani

Bathi Rabimu

jina la mji

Pua yako ni kama mnara wa Lebanoni

Pua yake ni ndefu na wima kama vile mnara uivyo mrefu na wima.

ambao watazama Damasko

"unao wawezesha watu kutazama kuelekea Damasko"

Song of Songs 7:5

Maelezo ya Jumla

Mpenzi anaendelea kumuelezea yeye anaye mpenda.

Kichwa chako ni kama Karmeli

Mwanamke analinganishwa na Mlima Karmeli ambao umeinuka kuliko kitu chochote karibu yake.

zambarau nyeusi

Tafsiri zinazo wezekana ni 1) "nyeusi iliyo koa" au 2) "nyekundu iliyo koa."

Mfalme amestaajabishwa na vifundo vyake

"Nywele zinazo ni'ng'inia ni nzuri hadi mfalme anashindwa kuacha kuzitamani."

vifundo

marundo ya nywele yanayo ni'ng'inia kutoka kichwani mwa mwanamke.

Song of Songs 7:7

Maelezo ya Jumla

Mpenzi anaelezea nini angependa kufanya kwa yeye anaye mpenda.

Urefu wako ni wa kama mti wa mtende

"Una simama kama mti wa mtende." Mwanamke ni mrefu, kasimama wima, na anavutia kama mti wa mtende.

mti wa mtende

mti mrefu wa wima unao zalisha matunda matamu ya rangi ya brauni yanayo ota kwa makundi

maziwa yako kama vifungu vya matunda

Mbegu katika mti wa mtende vinaota katika vifungu vizuri vinavyo teremka chini ya mti.

Ninataka kuupanda ... matawi yake

Mwanamme anataka kumshika mwanamke.

Maziwa yako nayawe kama vifungu vya mizabibu

Mwanamke anataka kushika maziwa yake yaliyo kaza lakini malaini kama mizabibu iliyo jawa na maji yake.

harufu ya pua yako yawe kama mapera

"harufu inayo toka kwenye pua yako inukie vizuri kama mapera."

mapera

Neno "mapera" la husu ladha ya tunda tamu, lenye rangi ya njano, aina nzuri ya tunda.

Song of Songs 7:9

Maelezo ya Jumla

Mpenzi anaendelea kueleza nini angependa amfanyie mwanamke.

Mdomo wako na uwe kama mvinyo bora

"Ninataka kuuonja mdomo wako kama mvinyo bora."

ukishuka taratibu kwa mpenzi wangu

Mpenzi anafurahia mabusu mororo ya mwanamke.

ukiteleza kwenye midomo yetu na meno

"unao shuka kwenye midomo yetu na meno"

Song of Songs 7:10

Mimi ni wa mpenzi wangu

Ona jinsi ulivyo tafsiri 6:2

na ananitamani

"na ana shauku juu yangu" au "ana nitaka"

Song of Songs 7:12

Maelezo ya Jumla

Mwanamke anaendelea kuzungumza na mpenzi wake.

Tuamke mapema

"inuka mapema" au "amka mapema"

imemea

"ipo katika mwanzo wa kustawi"

imechipua

maua yanapo funguka

imetoa mau

"maua kufunguka kwa mimea"

nitakupa penzi langu

"nitakuonyesha penzi langu" au "nitafanya mapenzi na wewe"

Song of Songs 7:13

Maelezo ya Jumla

Mwanamke anaendelea kuzungumza na mpenzi wake.

Mitunguja

Hili ni jina la mmea unao toa harafu kali lakini nzuri. Harufu kidogo ya lewesha na kuchochea hamu ya kufanya mapenzi.

ya toa harufu yake

"ya zalisha harufu yake"

katika mlango

Ina hashiria kuwa mlango ni wa nyumba yao.

kila aina ya matunda, mpya na ya kale

"kuna kila aina ya matunda mazuri, yaliyo mapya na ya zamani"

niliyo kuhifadhia

"kubakiza kwa ajili yako" au "kulinda kwa ajili yako"

Song of Songs 8

Song of Songs 8:1

kama kaka yangu

Mwanamke anatamani angemuonyesha mpenzi wake mahaba hadharani kama ngefanya kwa kaka yake. Hasemi kuwa mwanamke anaruhusiwa kufanya mapenzi na kaka yake.

ningekuona nje

"wewe hadharani"

ningekubusu

Mwanamke inawezekana anambusu kaka yake kwenye shavu kumsalimia.

kunidharau

"kunifanya nijisika haya"

Song of Songs 8:2

Maelezo ya Jumla

Mwanamke anaendelea kuzungumza na mpenzi wake.

Nitakuongoza na kukuleta kwenye nyumba ya mama yangu

Kama mpenzi angekuwa kaka yake, angemleta kwa nyumba ya familia. Hii ilikuwa kawaida katika huo utamaduni na bado unaendelea kwa baadhi.

na utanifundisha

Hii yaweza tafsiriwa kama "na ata nifundisha." Kwasababu mwanamke hana uzoefu wa kufanya mapenzi, ana fikiri kuwa mpenzi wake au mama yake angemfundisha jinsi ya kufanya mapenzi.

Nitakupa mvinyo ulio chachwa unywe na baadhi ya jwisi ya komamanga

Mwanamke anatumia haya maumbo kusema kuwa atajitolea kwa mpenzi wake na kufanya mapenzi naye.

mvinyo ulio chachwa

"mvinyo wenye viungo" au "mvinyo wenye viungo ndani yake" Hii ya wakilisha nguvu ya kulevya ya mapenzi.

jwisi ya komamanga

Mwanamke ana wakilisha kimiminika chake na maji ya komamanga.

Mkono wake wa kushoto...wanikumbatia

Tazama ilivyo tafsiriwa "Mkono wake wa kushoto upo chini ya kichwa changu, na mkono wake wa kulia wanikumbatia" ndani ya 2:5.

Song of Songs 8:4

Ninataka ... wanaume wa Yerusalemu

Ona jinsi ulivyo tafsiri 2:7

kuwa ... hadi yatakapo isha

Ona jinsi ulivyo tafsiri 2:7

Song of Songs 8:5

Maelezo ya Jumla

Hapa ni mwanzo wa Sehemu ya Sita ya kitabu, sehemu ya mwisho

Ni nani huyu anaye kuja

"Mwangalie huyu mwanamke wa ajabu anaye kuja." Ona jinsi ulivyo tafsiri maneno kama haya 6:10

nimekuamsha

"Nimekuamsha uamke"

mti wa mpera

Ona jinsi ulivyo tafsiri 2:3

pale

chini ya mpera

alijifungua wewe

alikuzaa

Song of Songs 8:6

Maelezo ya Jumla

Mwana mke anaendelea kuzungumza na mpenzi wake.

Nieka kama muhuri kwenye moyo wako, kama muhuri kwenye mkono wako

Maana zinazo wezekana ni 1) Kwasababu mihuri ilikuwa muhimu, watu waliweka shingoni mwao au mikononi mwao. Mwanamke anataka kuwa na mwanamme wake kama muhuri. Au 2) Muhuri waonyesha nani anamiliki kitu chenye muhuri wake. Mwanamke anataka awe kama muhuri moyoni mwa mpenzi wake na mkononi ili kuonyesha mawazo yake, hisia, na matendo ni yake.

kwa kuwa mapenzi yana nguvu kama mauti

Mauti ina nguvu sana kwasababu inawashinda ata watu wenye nguvu duniani.

hayana kurudi kama kwenda kuzimu

Kuzimu hakuruhusu watu kurudia uhai baada ya kuwa wamekufa. Mapenzi yana msimamo kama kuzimu kwasababu hayabadiliki.

miale yake yalipuka ... kuliko moto wowote

Mapenzi yana nguvu kama moto.

yalipuka

"kuchomeka ghafla"

Song of Songs 8:7

Maelezo ya Jumla

Mwanamke anaendelea kuongea na mpenzi wake.

Maji yalio zuka hayawezi kuzimisha upendo

Mpenzi yana nguvu kiasi kwamba ni kama moto mkali usio weza kuzimwa kwa bahari iliyo jawa na maji.

Maji yalio zuka

"Maji ya bahari" au "Kiasi kikubwa cha maji"

hayawezi kuzimisha

"hayawezi kutokomeza" au "hayawezi kuondoa"

wala mafuriko hayawezi kuondoa

Mapenzi kamwe hayabadiliki na ubaki hivyo daima ni kitu ambacho mafuriko yenye nguvu kiasi gani hayawezi kusogeza.

mafuriko

Katika Israeli, maji kutoka kwenye mvua utiririka mabonde marefu membamba. Hii ujenga mafuriko ya maji yenye nguvu kiasi cha kusogeza vizingiti vikubwa na miti. Ata leo mafuriko wakati mwengine uamisha madaraja imara sana.

kuondoa

"kubeba kando" au "kusafishia mbali"

Mwanaume akitoa ... ukarimu wake utadharauliwa

"Ata kama mwanaume ... ata dharauliwa sana."

mali zake zote

"vyote anavyo miliki"

kwa ajili ya upendo

"ili apate mapenzi" au "ili anunue mapenzi"

ukarimu wake utadharauliwa

"watu wata mdharau hakika" au "watu wata mdhihaki vikali"

Song of Songs 8:8

hatakayo ahidiwa kuolewa

"mwanamme anakuja na kutaka kumuoa"

Song of Songs 8:9

Maelezo ya Jumla

Kaka zake mwanamke wanaendelea kuongea miongoni mwao.

Kama ni ukuta ... mbao za mierezi

Kwasababu matiti yake ni madogo, ana kifua kitupu kama ukuta au mlango. Kaka zake wana amaua kumpa mapambo ili kumsaidia dada yao kuonekana mzuri zaidi.

tutampamba

"tuta mremba"

Song of Songs 8:10

matiti yangu sasa ni kama nguzo imara

matiti ya mwanamke ni marefu kama minara.

hivyo nimekomaa machoni pake

Mpenzi wake sasa anamuona ni mwanamke aliye komaa, na hilo la mpendeza.

machoni pake

Hapa "machoni pake" ya husu mpenzi wake.

Song of Songs 8:11

Baali Hamoni

Hili ni jina la mji kaskazini mwa Israeli.

wao ambao watalitunza

"watu watakao simamia"

Kila mmoja alipaswa kuleta shekeli elfu moja za fedha kwa matunda yake

"Kila mwanaume alipaswa kumpatia Sulemani shekeli elfu moja kama malipo ya matunda ya shamba la mizabibu.

kuleta shekeli elfu moja za fedha

"kuleta shekeli 1,000 za fedha"

Shamba langu ka mzabibu ni langu

"Mimi ndiye muhusika wa shamba langu la mizabibu." Mwanamke anajitaja kama shamba la mizabibu kama ilivyo 1:5

shekeli elfu moja ni za kwako, Sulemani mpenzi

Mwanamke ana mpatia bure faida ya mizabibu kwa Sulemani japo kuwa ni yake anaeza kumpa yeyote anayetaka.

Song of Songs 8:13

sauti yako

"kwa sauti yako"

Song of Songs 8:14

uwe kama paa au mtoto wa paa

Ona jinsi ulivyo tafsiri 2:16

milima ya manukato

Mwanamke anatumia hili umbo kukaribisha mpenzi wake amfurahie.

Isaiah 1

Isaiah 1:1

Maono ya Isaya ... ambayo aliyaona

"Hili ni Ono la Isaya ... ambalo Yahwe alimwonyesha" au "Hiki ndicho Mungu alichomwonyesha Isaya"

Amozi

Amozi alikuwa baba wa Isaya

Yuda na Yerusalemu

"Yuda" ina maana ya ufalme wa kusini mwa Israeli. "Yerusalemu" ulikuwa mji wake muhimu zaidi. "wale wanaoishi Yuda na Yerusalemu" au "watu wa Yuda na Yerusalemu"

katika siku za Uzia, Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda.

Hii ni lahaja na ina maana ya kipindi ambacho kila mfalme alitawala. Walitawala mmoja baada ya mwingine, na sio wote kwa kipindi kimoja. "Pale Uzia, Yothamu, Ahazi na Hezekia walipokuwa wafalme wa Yuda"

Isaiah 1:2

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza na watu wa Yuda katika mtindo wa shairi.

Sikieni, enyi mbingu, na sikilizeni, enyi nchi

Ingawa unabii huu ulikusudiwa kwa ajili ya watu wa Yerusalemu na Yuda kusikiliza, Isaya anafahamu hawatasikiliza. Maana zawezekana kuwa 1) anazungumza kwa kifupisho, kana kwamba "mbingu" na "nchi" zingeweza kusikiliza kile Yahwe alichosema, au 2) maneno "mbingu" na "nchi" ni mifano ya maneno na neno la ujumla kwa ajili ya viumbe vyote hai kila sehemu. "wewe ambaye unaishi katika mbingu ... wewe ambaye unaishi juu ya nchi"

Yahwe

Hili ni jina la Mungu ambalo alilifunua kwa watu wake katika Agano la Kale.

Nimewarutubisha ... haielewi

Maneno ambayo Yahwe alizungumza na ambayo Isaya anazungumza kwa Waisraeli kwa niaba ya Yahwe.

Nimewarutubisha na kuwakuza watoto

Yahwe anazungumza kana kwamba maneno yake yalikuwa chakula na kana kwamba Waisraeli walikuwa watoto wake. "Nimewatunza watu wanaoishi Yuda kama walikuwa watoto wangu"

punda kihori cha kulisha cha bwana wake

Unaweza kuiweka wazi taarifa inayoeleweka. "punda anajua kihori cha kulisha cha bwana wake" au "punda anajua ni wapi bwana wake humpatia chakula"

lakini Israeli haijui, Israeli haielewi

Yawezekana hii ina maana ya "lakini watu wa Israeli hawanijui, hawaelewi ya kuwa mimi ndiye ninayewatunza"

Israeli

Huu ni mfano wa maneno kwa ajili ya watu wa Israeli. Yuda ni sehemu ambayo ilikuwa taifa la Israeli. "watu wa Israeli"

Isaiah 1:4

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza na watu wa Yuda katika mtindo wa shairi.

Taifa, wenye dhambi

Maana zawezekana kuwa 1) Isaya anasema mambo mawili tofauti juu yao. "Taifa la Israeli, nyie wenye dhambi" au 2) anasema jambo moja tu kuhusu wao. "Taifa la wenye dhambi"

watu waliolemewa kwa udhalimu

Kitu kizito sana ambacho mtu anweza kubeba ni sitiari ya dhambi nyingi. "dhambi yao ni kama mfuko mzito juu ya mabega yao unaowafanya vigumu kwao kutembea"

mtoto wa waovu

Neno "mtoto" ni sitiari ya watu ambao hufanya kile wengine walichokwisha fanya. "watu ambao hufanya uovu ule ule wanaouona wengine wakifanya"

tenda mabaya

fanya mambo maovu

Wamemtelekeza Yahwe

"Wameondoka mbali kutoka kwa Yahwe"

wamemdharau

"wamekataa kutii" au "wamekataa kuheshimu"

Israel

Yuda ni sehemu ya iliyokuwa taifa la Israeli.

Wamejitenganisha kutoka kwake

Ingawa katika kipindi kimoja walikuwa marafiki, kwa sasa wanamtendea kana kwamba hawamjui.

Isaiah 1:5

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza na watu wa Yuda katika mtindo wa shairi.

Kwa nini bado mnapigwa? Kwa nini mnaasi zaidi na zaidi?

Isaya anatumia maswali haya kuwakaripia watu wa Yuda. Maswali haya yanaweza kutafsiriwa kama kauli. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Unaendelea kufanya mambo ambayo Yahwe anatakiwa kukuadhibu. Unaendelea kuasi dhidi yake"

mnapigwa

Hapa neno "mnapigwa" ina maana ya watu ambao huishi Yuda na kwa hiyo ni katika wingi.

Kichwa kizima kimeugua, moyo wote ni dhaifu

Sitiari hii inalinganisha taifa la Israeli na mtu ambaye amepigwa. "Wewe ni kama mtu ambaye kichwa chake kimejeruhiwa na ambaye moyo wake ni dhaifu" au "Wewe ni kama mtu ambaye akili na moyo wake wote ni mgonjwa"

Hakuna sehemu iliyodhuriwa

Hii inaweza kuwekwa katika hali ya chanya. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "kila sehemu ya kwako imejeruhiwa" au "mtu amejeruhi kila sehemu ya kwako"

vilikuwa havijafunikwa, safishwa, kufungwa bendeji, wala kutibiwa kwa mafuta

Sitiari hii inalinganisha adhabu ambayo Mungu amewapa Israeli na vidonda halisi. Inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "hakuna mtu aliyefunga, safisha, kufunga bendeji, au kuwatibu kwa mafuta"

Isaiah 1:7

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza na watu wa Yuda katika mtindo wa shairi.

Nchi yako imeharibiwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Wameharibu nchi yako" au "Adui zako wameharibu nchi yako"

Miji yako imeungua

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "wameunguza miji yenu"

mashamba yenu - mbele yenu, wageni wanaingamiza

"watu ambao si wa nchi yenu wenyewe wanaiba mazao kutoka kwenye mashamba yenu huku mkitazama"

uharibifu uliotelekezwa

"tupu na kuharibiwa". Msemo huu wa nomino dhahania unaweza kuelezwa kama misemo ya kitenzi. "wameangamiza nchi na hakuna mtu anayeishi pale"

kupinduliwa na wageni

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "wageni wamepindua nchi yako" au "jeshi la kigeni limeitwaa kabisa"

binti Sayuni amabaki

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Nimemuacha binti wa Sayuni"

binti Sayuni

"binti" wa mji ina maana ya watu wa mji. "Watu wa Sayuni" au "Watu wanaoishi Sayuni"

ameachwa kama kibanda cha shamba la mizabibu, kama kivuli katika bustani ya matango

Maana zawezekana kuwa 1) "amekuwa mdogo kama kibanda katika shamba la mizabibu au kivuli katika bustani ya matango" au 2) "ameachwa kwa mtindo ambao mkulima huacha kibanda katika shamba la mizabibu au kivuli katika bustani ya matango anapokuwa kamalizana nayo"

kama ... matango, kama mji uliozingirwa

Maana nyingine yaweza kuwa "kama ... matango. Yeye ni mji uliozingirwa"

Isaiah 1:9

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza na watu wa Yuda katika mtindo wa shairi.

Kama Yahwe

Hii inaelezea jambo amabalo lingeweza kutokea zamani lakini halikutokea.

mabaki wachache

"waliokoka wachache"

ametuachia ... tungekuwa

Hapa maneno haya yana maana ya Isaya na yanajumuisha watu wote wa Yuda na Yerusalemu.

tungekuwa kama Sodoma, tungekuwa kama Gomora

Jinsi ambavyo Yuda angekuwa kama Sodoma na Gomora inaweza kufanywa wazi. "Mungu angetuangamiza, kama alivyoangamiza miji ya Sodoma na Gomora"

Isaiah 1:10

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza na watu wa Yuda katika mtindo wa shairi.

nyie watawala wa Sodoma ... nyie watu wa Gomora

Isaya analinganisha watu wa Yuda na Sodoma na Gomora kusisitiza jinsi walivyokuwa wenye dhambi. "nyie watawala ambao mna dhambi kama watu wa Sodoma ... nyie watu ambao ni waovu kama wale walioishi Gomora"

"Wingi wa sadaka zako kwangu ni upi?"

Mungu anatumia swali kukaripia watu. Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Sadaka zako nyingi hazina maana yoyote kwangu!"

Isaiah 1:12

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza maneno ya Yahwe kwa watu wa Yuda katika mtindo wa shairi.

ni nani ametaka kutoka kwako, kukanyaga mahakama yangu?

Neno "kukanyaga" lina maana ya kukanyaga juu ya na kuponda kwa mguu wa mtu. Mungu anatumia swali kukaripia watu wanaoishi Yuda. Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "hakuna aliyekuambia kukanyanga katika uwanja wangu wa mahakama!"

Usilete sadaka zisizo na maana

"Usiniletee zawadi zako zaidi zisizo na maana"

ubani ni chukizo kwangu

Hapa nomino dhahania ya "chukizo" inaweza kuelezwa kama kitenzi "chuki". "Ninachukia ubani makuhani wanayochoma"

siwezi kustahimili mikusanyiko hii ya kiovu

Maana zawezekana kuwa 1) "Siwezi kuwaruhusu kukusanyika pamoja kwa sababu ya mambo maovu mnayofanya" au 2) "Siwezi kujiruhusu kuwatazama mkikusanyika pamoja kwa sababu ya mambo maovu mnayofanya"

Isaiah 1:14

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza maneno ya Yahwe kwa watu wa Yuda katika mtindo wa shairi.

mbala miezi yenu mipya, na sikukuu mlizochagua

Maneno "mbala miezi mipya" ni mfano wa maneno kwa sherehe za mwezi mpya. Pia ni maneno yenye maana sawa na sherehe za kawaida. "sherehe zako za mbala miezi mipya na sikukuu zingine mpya"

mbala miezi mipya

Mbala mwezi mpya ni pale ambapo mwezi unapoanza kutoa mwanga baada ya kuwa giza.

ni mzigo kwangu; nimechoka kivivumilia

Hii inalinganisha namna Mungu anavyojisikia kuhusu sherehe za watu kwa kubeba kitu kizito. "wao ni mzigo mzito ambao nimechoka kuubeba"

ninaficha macho yangu kwako

Lahaja hii niu njia ya kusema "Sitakutazama" au "Sitakutazama kwa uangalifu"

mikono yako imejaa damu

Hii ni sababu ambayo Mungu hatasikia maombi yao. Damu inawezekana kumaanisha vurugu ambayo wamefanya dhidi ya watu. "kwa sababu ni kama mikono yako imefunikwa na damu ya wale uliowadhuru" au "kwa sababu una hatia ya vurugu"

Isaiah 1:16

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza maneno ya Yahwe kwa watu wa Yuda katika mtindo wa shairi.

Jioshe, jisafishe

Hapa Mungu analinganisha mtu anayeacha kutenda dhambi na mtu ambaye anaosha mwili wake. "Tubu na uoshe dhambi kutoka moyoni mwako kama uanvyoosha uchafu kutoka mwilini mwako"

ondoa uovu wa matendo yako kutoka machoni pangu

Mungu hakuwa anawaambia kufanya matendo yao maovu sehemu nyingine, lakini kuacha kuyafanya. "acha kufanya matendo maovu ambayo naona mnafanya"

nyosha wima ukandamizaji

Mungu anazungumza na watu ambao huwakandamiza wengine kana kwamba wamefanya kitu kupinda ambacho kilitakiwa kuwa wima, na anawaita kukifanya kitu hicho kuwa wima tena. Nomino dhahania "ukandamizaji" inaweza kutafsiriwa kama kitenzi. "hakikisha ya kwamba wale watu wasiojiweza uliowadhuru hawateseki kutoka na mambo mabaya uliyofanya kwao"

toa haki kwa yatima

"uwe na haki kwa watoto ambao hawana baba"

walinde wajane

"walinde wanawake ambao waume zao wamefariki"

Isaiah 1:18

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Yuda.

Njooni sasa, na

Yahwe anawakaribisha kwa upendeleo na upendo watu kusikiliza kile anachotaka kusema. "Tafadhali mnisikilize. Na" au "Zingatia kwa makini; Ninataka kukusaidia".

tutafakari pamoja

"Tufikirieni juu ya hili pamoja" au "tunahitaji kujadili hili" au "tutaenda kufanya nini?". Yahwe anawakaribisha watu kujadili siku za usoni. Hapa neno "tutafakari" lina maana ya Yahwe na linajumuisha watu wa Yuda.

ingawa dhambi zako ni rangi nyekundu, zitakuwa nyeupe kama theluji; ingawa ni nyekundu kama nyekundu iliyoiva, zitakuwa kama sufu

Isaya anazungumza na watu kana kwamba walikuwa wanavaa nguo ambazo zilitakiwa kuwa sufu nyeupe na dhambi zao kana kwamba zilikuwa mabaka mekundu ya dhambi juu ya nguo. Iwapo Yahwe anasamehe dhambi zao, itakuwa kana kwamba nguo zao zitakuwa nyeupe tena.

ni rangi nyekundu

Rangi nyekundu ni rangi nyekundu inayong'aa "nyekundu inayong'aa"

nyeupe kama theluji

Nyeupe mara kwa mara ni alama ya utakatifu au usafi. "Theluji" ina maana ya kitu kama mvua iliyoganda ambayo ni nyeupe sana. Kwa kuwa hii

nyekundu iliyoiva

Nyekundu hii ni nyekundu iliyoiva "nyekundu iliyoiva"

kama sufu

Sufu ni manyoya ya kondoo au mbuzi. Jinsi zitakavyokuwa kama sufu inaweza kufanywa wazi. "nyeupe kama sufu"

Isaiah 1:19

Taarifa ya Jumla

Mungu anaendelea kuzungumza na watu wa Yuda.

Kama u mtiifu na tayari

Hapa, "tayari" na "mtiifu" inatumika pamoja kumaanisha wazo moja. "Kama upo tayari kutii"

utakula mema ya nchi

"nchi itazaa chakula kizuri kwa ajili yako kula"

lakini kama utakataa na kuasi

"lakini kama ukikataa kusikiliza na badala yake kutonitii mimi"

upanga utakumeza

Neno "upanga" lina maana ya maadui wa Yuda. Pia, neno "kumeza" inalinganisha maadui wa Yuda kuja kuwaua kama mnyama pori ambaye hushambulia na kula wanyama wengine. "maadui wako watakuua"

kinywa cha Yahwe kimesema hivi

Neno "kinywa" kinasisitiza ya kwamba Yahwe amasema na kile anachosema hakika kitatokea. "Yahwe amezungumza" au "Yahwe amesema ya kwamba hiki kitatokea"

Isaiah 1:21

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza na watu wa Yuda katika mtindo wa shairi.

Jinsi mji mwaminifu

Neno hili la mshangao linaonyesha hasira na huzuni ya Isaya juu ya watu wa Yerusalemu. "Tazama jinsi watu wa Yerusalemu, ambao wamekuwa waaminiufu kwa Mungu"

ulivyokuwa kahaba

Isaya analinganisha watu na mwanamke ambaye sio mwaminifu kwa mumewe lakini analala na wanamume wengine kwa pesa. Watu hawakuwa waaminifu kwa Mungu lakini walikuwa wakiabudu miungu ya uongo. "kutenda kama kahaba"

Alikuwa amejaa haki

Neno "alikuwa" ina maana ya Yerusalemu na watu wake. Wale waliondika Biblia mara kwa mara walimaanisha miji kama wanawake. "Watu wa Yerusalemu walikuwa wa haki na walifanya kilicho sahihi"

lakini sasa amejaa wauaji

Neno "amejaa" lina maana ya Yerusalemu na watu wake. Wale waliondika Biblia mara kwa mara walimaanisha miji kama wanawake. "lakini sasa watu wa Yerusalemu ni wauaji"

Fedha yako imekuwa chafu, divai yako imechanganywa na maji

Maana zawekekana kuwa ya kwamba Isaya anatumia fedha na divai kama sitiari ya 1) watu wa Yerusalemu. "Wewe ni kama fedha ambayo sio safi tena, na kama divai ambayo imechanganywa na maji" au 2) matendo mema ambayo watu walifanya awali. "Mlikuwa mkifanya matendo mema, lakini sasa matendo yenu mabaya yanafanya matendo yenu mema kutokuwa na maana".

fedha ... chafu

Mtu huhitaji kusafisha fedha mara kwa mara au haitang'aa tena.

divai ... maji

Divai na maji ndani yake ina ladha kidogo na kwa hiyo haitofautiani na maji.

Isaiah 1:23

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza maneno ya Yahwe kwa watu wa Yuda katika mtindo wa shair.

Wakubwa wenu ni waasi

"Viongozi wao wanaasi dhidi ya Mungu"

wenzi wa wezi

"wao ni marafiki wa watu ambao huiba kutoka kwa wengine"

rushwa ... malipo

Watu hutoa "rushwa" kama zawadi kwa watawala wasio waaminifu kwa hiyo watawala hapohapo watatenda kinyume na haki. Watawala hupokea "malipo" kama zawadi kutoka kwa wale hutengeneza faida kutoka kwa sheria zisizo haki ambazo mtawala amezipitisha.

hukimbilia malipo

Mtu anapokuwa na shauku sana mtu ampatie rushwa inazungumzwa kana kwamba malipo yanakimbia na mtu anayafukuza. "kila mtu hutamaniu mtu kumlipa pesa kufanya maamuzi yasiyo ya kweli"

Hawawalindi yatima

"hawawalindi wale ambao hawana baba"

wala maombi ya haki ya mjane hajaji mbele zao

"wala hawasikii pale ambapo wajane huenda kwao kupata msaada dhidi ya wale wanaovunja sheria" au "na hawasaidii wajane wanaokwenda kwao kupata msaada dhidi ya wale wanaovunja sheria"

Isaiah 1:24

Taarifa ya Jumla

Isaya anaanza kuzungumza maneno ya Yahwe kwa watu wa Yuda katika mtindo wa shairi.

Kwa hiyo

"Kwa sababu hiyo"

Hili ni tamko la Mungu

Nomino dhahania "tamko" inaweza kutafsiriwa kama kitenzi. "hivi ndivyo ambavyo Mungu anatamka"

Nitafanya kisasi dhidi ya washindani wangu, na kujilipiza kisasi dhidi ya adui zangu

Misemo hii miwili kimsingi ina maana moja. Maneno "chukua kisasi dhidi ya maadui wangu" huzungumza zaidi juu ya Yahwe kufanya chochote anachohitaji kufanya kwa wale wanaofanya kazi dhidi yake ili aweze kuwa na furaha. Maneno "kujilipiza kisasi dhidi ya adui zangu" yanazungumza zaidi juu ya Yahwe kuadhibu kwa haki adui zake. "Nitaadhibu wale ambao wananipinga" au "Nitafanya kile kinachonipendeza kwa wale wanaofanya kazi dhidi yangu, na nitaadhibu kwa haki adui zangu"

Nitageuza mkono wangu dhidi yako

Hapa "mkono" ina maana ya nguvu ya Mungu ambayo angetumia kuadhibu watu wake. "Nitaanza kutumia nguvu yangu yote dhidi yako"

safisha takataka zako kwa maji magadi

Hapa hatua ambayo Mungu hutoa dhambi za watu wake inazungumziwa kana kwamba anatenganisha chuma kutoka kwa vitu vibaya vilivyochanganywa navyo. Maneno "kwa maji magadi" yanaongeza sitiari nyingine, kwa sababu maji magadi hutumika ndani ya sabuni, sio kusafisha chuma. "na kama vile moto unavyotoa uchafu kutoka kwa fedha, nitatoa uovu wote kutoka miongoni mwao"

takataka

Huu ni uchafu na mambo mengine ambayo watu hutoa kutoka kwenye vyuma ili chuma kiwe safi.

Isaiah 1:26

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza na watu wa Yuda katika mtindo wa shairi.

hapo mwanzo ... hapo mwanzo

Hizi ni njia mbili za kuzungumzia sehemu ya kwanza au mwanzo wa historia ya Israeli, pale ambapo Israeli ilipokuwa taifa.

utaitwa

Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "watu watakuita"

mji wa utakatifu, mji mwaminifu

Hapa "mji" una maana ya watu wanaoishi Yerusalemu. "mji ambao watu ni watakatifu na waaminifu kwa Mungu"

Isaiah 1:27

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza maneno ya Yahwe kwa watu wa Yuda katika mtindo wa shairi.

Sayuni itakombolewa kwa haki, na waliotubu kwa utakatifu

Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. Maana zawezekana kuwa 1) " Yahwe atakomboa Sayuni kwa sababu watu pale hufanya kilicho haki, na atawakomboa wale wanaotubu kwa sababu wanafanya kile ambacho Yahwe anasema ni sahihi" au 2) "Yahwe atakomboa Sayuni kwa sababu ana haki, na atakomboa wale wanaotubu kwa sababu ni mtakatifu"

Sayuni

Huu ni mfano wa maneno wa "watu wanaoishi juu ya Mlima Sayuni".

Waasi na wenye dhambi wakandamizwa pamoja

Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "Mungu ataangamiza wale ambao huasi na kutenda dhambi dhidi yake"

wale wanaomuacha Yahwe watatoweka kabisa

Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "na Yahwe atawaondoa kabisa wale wanaogeuka kutoka kwake" au "na Yahwe atawaua wote wanaomkataa"

Isaiah 1:29

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza maneno ya Yahwe kwa watu wa Yuda katika mtindo wa shairi.

Miti ya mwaloni mitakatifu ... bustani

Misemo hii ina maana ya sehemu ambapo watu wa Yuda waliabudu sanamu.

utaaibika kwa

Baadhi ya tafsiri husema, "utaona aibu kwa sababu ya". Mtu huona aibu uso wake unapochemka, mara kwa mara kwa sababu anahisi amefanya kitu kibaya.

Kwa maana utakuwa kama mwaloni ambao majani hufifia, na kama bustani ambayo haina maji

Maji hutoa uhai kwa miti na bustani. Watu wamejikata kutoka kwa Yahwe, ambaye hutoa uhai.

Isaiah 1:31

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza maneno ya Yahwe kwa watu wa Yuda katika mtindo wa shairi.

Mtu mwenye nguvu

"Mtu mwenye nguvu" au "Yeyote mwenye nguvu". Hii inaweza kumaanisha watu ambao ni muhimu na wana ushawishi kwa watu wengine"

vitu vinavyoshika moto haraka

vitu vilivyokauka vinavyowaka kirahisi

na kazi yake kama cheche

Hii inalinganisha matendo ya mtu au kazi zake za uovu na cheche ambazo huanguka juu ya vitu vinavyoshika moto haraka na kuiwasha moto. "kazi yake itakuwa kama cheche ambayo huanzisha moto"

Isaiah 2

Isaiah 2:1

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza na watu wa Yuda katika mtindo wa shairi.

Yuda na Yerusalemu

"Yuda" na "Yerusalemu" ni mifano ya maneno kwa ajili ya watu wanaoishi pale. "wale wanaoishi katika Yuda na Yerusalemu"

katika siku za mwisho

"katika siku za usoni"

mlima wa nyumba ya Yahwe utaimarishwa

Hii inaweza kuwekwa 1) kama ufafanuzi. "Mlima wa nyumba ya Yahwe utasimama" au 2 katika hali ya kutenda. "Yahwe ataimarisha mlima ambapo hekalu lake linajengwa"

kama kilele cha milima

Isaya anazungumzia umuhimu kana kamba ni urefu wa kihalisia. "sehemu muhimu zaidi ya milima" au "sehemu muhimu zaidi duniani"

itainuliwa juu zaidi ya vilima

Isaya anazungumzia heshima kama sitiari kana kwamba ilikuwa urefu halisi. Hii inaweza kuwekwa 1) katika hali ya kutenda. "Yahwe atuheshimu kuliko kilima kingine" au 2) kama mfano wa maneno kwa ajili ya watu wanaoabudu pale. "Yahwe atawaheshimu watu ambao wanaabudu pale kuliko vile anavyoheshimu watu wengine wowote"

na mataifa yote

Hapa "mataifa" ni mfano wa maneno kwa ajili ya watu wa mataifa hayo. "na watu kutoka mataifa yote"

yatatiririka kwake

Watu kuzunguka duniani kwenda katika mlima wa Yahwe inalinganishwa na jinsi mto unavyotiririka. Hii inasistiza ya kuwa watu wengi watakuja, sio tu watu wachache.

Isaiah 2:3

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza na watu wa Yuda katika mtindo wa shairi.

Yakobo, ili aweze kufundisha ... na tuweze kutembea

Maana nyingine ni "Yakobo . Atafundisha ... na tutatembea"

aweze kutufundisha baadhi ya njia zake, na tuweze kutembea katika njia zake

Neno "njia" ni sitiari kwa namna mtu anavyoishi. Kama lugha yako ina neno moja tu kwa ardhi ambayo watu wanatembea, unaweza kunganisha miseo hii miwili. "aweze kutufundisha mapenzi yake ili kwamba tuweze kumtii"

Kwa maana kutoka kwa Sayuni sheria itakwenda, na neno la Yahwe kutoka Yerusalemu

Misemo hii ina maana ya kitu kiimoja. Isaya alikuwa akisisitiza ya kwamba mataia yote yataelewa ya kwamba ukweli unapatikana Yerusalemu. "Watu wa Sayuni watafundisha sheria ya Mungu, na watu wa Yerusalemu watafundisha neno la Yahwe"

Kwa maana kutoka kwa Sayuni sheria itakwenda

"Kwa maana sheria itakwenda kutoka Sayuni". Isaya anazungumza kana kwamba sheria ilikuwa kitu kama mto ambao husogea bila watu kufanya lolote. "Wale ambao wanafundishwa sheria watatoka nje kutoka Sayuni" au "Yahwe atatangaza sheria yake kutoka Sayuni"

neno la Yahwe kutoka Yerusalemu

"neno la Yahwe litatoka kutoka Yerusalemu". Isaya anazungumza kana kwamba neno la Yahwe lilikuwa kitu kama mto ambacho kinasogea bila watu kufanya lolote. Unaweza kufanya taarifa inayoeleweka wazi. "Wale ambao wanafundishwa sheria watatoka nje kutoka Yerusalemu" au "Yahwe atatangaza sheria yake kutoka Yerusalemu"

Isaiah 2:4

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza na watu wa Yuda katika mtindo wa shairi.

Atawahukumu

"Yahwe atawahukumu"

atatoa maamuzi

"atatatua ugomvi"

watatwanga panga zao katika majembe, na mikuki yao katika ndoano za kupogolea

Watu wa mataiufa watageuza silaha zao za vita kuwa vifaa kwa ajili ya ukulima.

panga ... mikuki ... upanga

Maneno haya ni maana sawa ya silaha za aina yoyote.

majembe ... ndoano za kupogolea

Maneno haya ni maana sawa ya vifaa vya aina yoyote ambavyo watu hutumia katika shughuli za amani.

watatwanga panga zao katika majembe

"watafanya panga zao kuwa vifaa kwa ajili ya kuoanda mbegu". Jembe ni ubapa ambao watu hutumia kuchimba katika ardhi iuli waweze kupanda mbegu pale.

na mikuki yao katika ndoano za kupogolea

"watatwanga mikuki yao kuwa ndoano za kupogolea" au "watafanya mikuki yao kuwa vifaa kwa kutunza mimea". Ndoano ya kupogolea ni kisu ambacho watu hutumia kukata matawi ambayo hayahitajiki kutoka kwa mimea.

taifa halitainua panga lake dhidi ya taifa

"hakuna taifa litainua panga lake dhidi ya taifa lingine". Panga ni mfano wa maneno kwa ajili ya vita. "taifa moja halipigana vita dhidi ya taifa lingine"

wala hatafanya maandalizi kwa ajili ya vita

"wala hawatafanya maandalizi kupigana vitani". Mwandishi anatarajia msomaji kuamiini ya kwamba wale wanaopigana vita hufanya maandalizi kabla ya kupigana na kwamba baadhi wanaofanya maandalizi hawapigani.

Isaiah 2:5

Taarifa ya Jumla

Katika 2:5 Isaya anazungumza na watu wa Yuda, na katika 2:6 anazungumza na Yahwe. Nyakati zote mbili anazungumz katika mtindo wa shairi.

Nyumba ya Yakobo

"Nyie uzao wa Yakobo". Neno "nyumba" ni mfano wa maneno kwa ajili ya watu wanaoishi katika nyumba, familia. Hapa "Yakobo" inawakilisha taifa la Yuda, lakini itafaa zaidi kutumia "Yakobo" hapa.

njooni

kutumainisha kwa upole kufanya kile mwandishi anataka kumwambia msikilizaji kufanya.

na tutembee katika nuru ya Yahwe

Isaya anazungumza na watu kujifunza na kisha kufanya kiile Yahwe anachotaka wao kufanya kana kwamba walikuwa wakitembea usiku na nuru ambayo Yahwe aliwapatia ili waweze kuona njia. "na tujifunze jinsi Yahwe anatutaka tuishi na kisha tuishi namna hiyo"

Kwa kuwa mmetelekeza watu wako

"Kwa kuwa mmewaacha watu wako" na haujali nini kitatokea kwao. Hapa neno "mmetelekeza" lina maana ya Yahwe ni kwa hiyo ni katika umoja.

wamejazwa kwa tamaduni kutoka mashariki

Isaya anazungumza kana kwamba watu walikuwa vyombo ambavyo vilikuwa vimejaa na kitu kutoka mashariki. Maana zaweza kuwa anazungumza 1) matendo ambayo watu wa mashariki hufanya. "wanafanya kila wakati matendo maovu ambayo watu wanaoishi katika nchi za mashariki mwa Israeli hufanya" au 2) watu, haswa wale wanaotangaza kuzungumza na wafu, ambao wanatoka mashariki kufanya matendo maovu. "waaguzi wengi wanatoka mashariki na sasa wanaishi pale"

wasoma ishara

watu wanaotangaza ya kwamba wanaweza kutabiri muda ujao kwa kutazama vitu kama sehemu ya wanyama na majani.

na wanashika mikono na wana wa wageni

Kushika mikono pamoja ni ishara ya urafiki na amani. "wanafanya amani na kufanya kazi pamoja na watu ambao hawatoki Israeli"

Isaiah 2:7

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza na Yahwe katika mtindo wa shairi.

Nchi yao imejaa fedha ... nchi yao pia imejaa farasi ... Nchi yao pia imejaa sanamu

Isaya anazungumza kana kwamba nchi ilikuwa chombo ambacho mtu ameweka fedha, farasi, na sanamu. Neno "nchi" ni mfano wa maneno kwa ajili ya watu wenyewe, na maneno "imejaa" ni sitiari kwa ajili ya watu kumiliki vifaa hivi. "Wanamiliki fedha nyingi ... pia wanamiliki farasi nyingi ... Pia wanamiliki sanamu nyingi"

ufundistadi wa mikono yao wenyewe, vitu ambavyo vidole vya wenyewe vimetengeneza

Misemo hii miwili ina maana moja na inasisitiza ya kwamba hivi sio miungu ya kweli. Kama lugha yako haina maana ya jumla kwa kitu ambacho mtu ametengeneza, unaweza kuunganisha misemo hii miwili katika moja. "vitu ambavyo wao wenyewe umetengeneza"

ufundistadi wa mikono yao wenyewe

Neno "mikono" ina maana sawa na watu wenyewe. "ufundistadi wao wenyewe" au "kazi yao wenyewe" au "vitu ambavyo wametengeneza kwa mikono yao"

vitu ambavyo vidole vya wenyewe vimetengeneza

Neno "vidole" ina maana sawa na watu wenyewe. "vitu ambavyo wametengeneza kwa vidole vyao wenyewe"

Isaiah 2:9

Taarifa ya Jumla

Katika 2:9 Isaya anamaliza kuzungumza na Yahwe. Katika 2:10-11 Isaya anazungumza na watu wa Yuda. Nyakati mbili anazungumza katika mtindo wa shairi.

Watu watainamishwa, na kila mtu binafsi ataanguka chini

Hapa kuwa chini mpaka ardhini inawakilisha watu ambao wameaibishwa kabisa kwa sababu wamegundua yote waliyoamini hayana maana, na hawawezi kufanya kitu kujisaidia wenyewe. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "'Mungu atafanya watu waaibike, na watagundua ya kwamba waliamini katika vitu visivyo na maana"

Watu

binadamu, tofauti na wanyama

mtu binafsi

"kila mtu"

usiwainue juu

Maneno "kuwainua juu" ni sitiari kwa ajili ya Yahwe kusamehe watu. "usiwasamehe"

Nenda katika sehemu za mawe

Maana zaweza kuwa watu wanapaswa kwenda katika 1) mapango juu ya teremko za upande wa milima au 2) sehemu ambapo kuna mawe makubwa mengi ambapo mtu atajificha.

jifiche katika ardhi

Maana zaweza kuwa ya kwamba watu wanapaswa kujificha 1) katika shimo la kawaida katika ardhi au 2) katika shimo ambalo wanachimba katika ardhi.

kutoka kwa hofu kuu ya Yahwe

Hapa nomino dhahania "hofu kuu" inaweza kuelezwa na kitenzi "kuogofya". "kutoka kwa uwepo wa kuogofya wa Yahwe" au "Kutoka kwa Yahwe kwa sababu utamwogopa sana"

utukufu wa ufalme wake

"uzuri wake mkuu na nguvu ambayo anayo kama mfalme" au "ufahari wake wa kifalme"

mtazamo wa kiburi wa mwanamume kutashushwa chini

"Yahwe atashusha chini mtazamo wa kiburi wa mwanamume". Mwanamume mwenye "mtazamo wa kiburi" anatazama juu ya kila mtu kuwaonyesha ya kwamba ni bora kuliko wao. Hapa watu wote wana hatia ya kufikiri wapo bora kuliko Yahwe, na jinsi wanavyotazama wale wanaomwabudu Yahwe, ni mfano wa maneno wa kiburi chao. "Yahwe atawaibisha watu wote kwa sababu wanafikiri wako bora kuliko yeye"

kiburi cha wanamume kutashushwa chini

Yahwe atawafanya wanamume wenye kiburi kuaibiika wao wenyewe. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe atashusha chini kiburi cha wanamume" "Wanamume wenye kiburi" ni mfano wa maneno wa watu wenye kiburi. "Yahwe atawashusha chini watu wenye kiburi"

Yahwe peke yake atainuliwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "watu watamsifu Yahwe tu"

katika siku hiyo

Hii ni lahaja. "katika siku ambayo Yahwe anahukumu kila mtu"

Isaiah 2:12

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza na watu wa Yuda katika mtindo wa shairi.

ambaye ana kiburi na ameinuliwa

Yule ambaye "ameinuliwa" ana majivuno na kujichukulia kuwa bora kuliko watu wengine. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "ambaye anajisifu na anajiinua juu ya watu wengine" au "ambaye anajivuna na kufikiri ya kwamba yuko bora kuliko watu wengine"

ambaye ana kiburi ... ambaye anajisifa

Mtu ambaye ana majivuno anaongeza na kutenda kana kwamba yupo bora kuliko watu wengine. Misemo hii miwili ina maana moja na inatumika pamoja kusisitiza ya kwamba Yahwe atawaadhibu wao"

na yeye atashushwa chini

"na kila mtu mwenye kiburi atashushwa chini". Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe atamnyenyekeza"

dhidi ya mierezi ya Lebanoni ... dhidi ya mwaloni ya Bashani

"Siku ya Yahwe wa Majeshi" itakuwa dhidi ya mierezi na mwaloni. Maana zaweza kuwa 1) miti hii ni sitiari kwa watu wenye kiburi ambao Mungu atawahukumu au 2) Mungu kwa uhakika ataangamiza miti hii mikuu.

Isaiah 2:14

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza na watu wa Yuda katika mtindo wa shairi. Anaendelea kufafanua kile kitakachotokea katika siku ya Yahwe wa Majeshi.

na dhidi ya

Katika 2:14-16 Isaya anaorodhesha viitu ambavyo Mungu ataangamiza. Maana zaweza kuwa 1) hivi vina maana ya watu wenye kiburi ambao Mungu atawashusha au 2) Mungu atawaangamiza kabisa vitu hivi katika orodha.

milima ... vilima

Maneno haya ni sitiari kwa ajilii kiburi cha Waisraeliu. Pia zinajitokeza katika 2:1.

ambayo imeinuliwa juu

Hii ni lahaja. "ambayo iko juu sana"

mnara wa juu ... ukuta usioshindika

Hii ina maana ya vitu ambavyo watu watajenga kuzunguka miji yao ilii waweze kujilinda dhidi ya adui zao. Ni sitiari kwa ajili ya kiburi cha Waisraeli na waliamini hawakuwa na hitaji la Yahwe na wangeweza kusimama dhidi ya adhabu yoyote Yahwe angewapimia kwao kwa ajili ya dhambi zao.

ukuta usioshindika

"ukuta ambao hakuna kitu kinachoweza kuvunja au kupita katikati"

meli za Tarshishi ... vyombo vizuri vya matanga

Hizi zina maana ya meli kubwa ambazo watu walitumia kusafiri mbali juu ya bahari na kuleta bidhaa katika miji yao.

meli za Tarshishi

"meli ambazo wanatumia kwenda Tarshishi"

Isaiah 2:17

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza na watu wa Yuda katika mtindo wa shairi. Anaendelea kufafanua kile kitakachotokea katika siku ya Yahwe wa Majeshi.

Kiburi cha mtu kitashushwa chini

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Atawashusha chini watu wenye kiburi" au "Atamuwaibisha kila mwanamume mwenye kiburi"

Kiburi cha wanamume kitaanguka

Nomino dhahania "kiburi" inaweza kutafsiriwa kama kivumishi. "wale watu ambao wana kiburi na wataacha kuwa na kiburi"

Yahwe pekee ayainuliwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "watu watamsifu Yahwe tu"

Hizo sanamu zitapita mbali kabisa

"Sanamu zote zitatoweka" au "Hapatakuwa na sanamu zaidi"

Wanamume watakwenda ... kutoka kwa hofu kuu

Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "Wanamume watakwenda .. kujificha kutoka kwa hofu kuu"

mapango ya mawe

"mapango katika mawe". Haya ni mawe makubwa, sio mawe madogo ambayo yanaweza kushikiliwa katika mkono.

kutoka kwa hofu kuu ya Yahwe, na kutoka kwa utukufu wa ukuu wake wa enzi

Hapa nomino dhahania "hofu kuu" inaweza kuelezwa na kitenzi "kuogofya". "kutoka kwa uwepo wa kuogofya wa Yahwe" au "Kutoka kwa Yahwe kwa sababu utamwogopa sana"

kutoka kwa hofu kuu ya Yahwe

kwa sababu walikuwa wanamuogopa sana Yahwe

kutoka kwa utukufu wa ufalme wake

Hapa neno "utukufu" kufafanua "ufalme". "uzuri ambao anao kama mfalme"

atakapoinuka kuogofya dunia

"pale Yahwe atakapochukua hatua na kusababisha watu wa dunia kumuogopa sana"

Isaiah 2:20

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza na watu wa Yuda katika mtindo wa shairi. Anaendelea kufafanua kile kitakachotokea katika siku ya Yahwe wa Majeshi.

kwa fuko na popo

Fuko ni wanyama wadogo ambao huchimba na kuishi chini ya ardhi. Popo ni wanyama wanaopaa wadogo ambao mara nyingi huishi ndani ya mapango. "kwa wanyama"

mianya katika mawe .. nyufa za mawe yaliyopasuka

Kama lugha yako haina maneno mawili tofauti kwa ajili ya "mianya" na "nyufa", nafasi inayojitokeza katikati ya sehemu mbili ya jiwe linapogawanyika, unaweza kuunganisha misemo hii miwili kuwa moja.

kutoka kwa hofu kuu ya Yahwe

kwa sababu walikuwa wakuimuogopa sana Yahwe.

utukufu wa ukuu wake wa enzi

"uzuri wake mkuu na nguvu ambayo anayo kama mfalme" au "ukuu wake wa enzi wa kifalme"

atakapoinuka kutisha dunia

"pale Yahwe anapochukua hatua na kusababisha watu wa dunia kumuogopa sana"

ambaye pumzi yake ya uhai ipo katika pua zake

pumzi ipo ndani ya pua zake Pua ni dhaifu na shimo za pua ni nzuri, kwa hiyo pia ni mfano wa watu, ambao ni dhaifu. "ni nani ambaye ni dhaifu na atakufa" au "nani anahitaji pumzi katika pua yake kuishi"

pua

mashimo katika pua ambapo watu hupumulia

kwa maana ataambulia wapi?

Isaya anatumia swali kuwakumbusha watu kitu ambacho wanapaswa kuwa wanakijua tayari. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli. "kwa maana mtu ataambulia patupu!" au "kwa maana mtu hana faida yoyote!"

Isaiah 3

Isaiah 3:1

Tazama

Neno "tazama" hapa linaongeza msisitizo kwa kile kinachofuata. Pia inaweza kutafsiriwa kama "Sikiliza" au "Hasa".

tegemeo na nguzo

Maneno haya mawili yana maana ya fimbo ya kutembelea, ambayo mtu huegemea kwa msaada. Wazo hili lina maana ya vitu ambavyo watu wanahitaji zaidi ili waishi: chakula na maji. "kila kitu ambacho kinakukimu" au "kila kitu ambacho unategemea"

mtu hodari ... mchawi wa kiume mwenye ujuzi

Hii ni orodha ya makundi ya watu ambao wengine wanawategemea. Kwa kuwa hazimaanishi watu binafsi hasa, inaweza kutafsiriwa na nomino za wingi. "wanamume hodari

msoma ishara

Hawa ni watu ambao wanadai ya kwamba wanaweza kujua mambo yajayo kwa kuangalia vitu kama sehemu za wanyama na majani.

nahodha wa hamsini

Hii lahaja ina maana ya nahodha ambaye anasimamia wanajeshi hamsini. Inaweza kutafsiriwa kwa msemo wa jumla zaidi. "afisa wa jeshi" au "jemadari wa jeshi"

hamsini

"50"

Isaiah 3:4

Nitaweka vijana wadogo kuwa viongozi wao, na watoto watatawala juu yao

Misemo hii ina maana ya kitu kimoja. Maana zaweza kuwa 1) "Nitaweka watu wachanga kama viongozi wao, na hao watu wachanga watatawala juu yao" au 2) "vijana" ni sitiari kwa ajili ya wanamume wapumbavu. "Nitawawekea juu yao viongozi ambao hawajakomaa, kama watu wachanga, na wale viongozi wabaya watatawala juu yao"

Nitaweka vijana wa kawaida

Hapa neno "Nitaweka" ina maana ya Yahwe. Hii inaweza kuwekwa wazi. "Yahwe anasema, "Nitaweka vijana wa kawaida kama viongozi wao""

Watu watakandamizwa, kila mmoja kwa mwingine, na kila mmoja kwa jirani yake

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Kila mtu atakuwa mkatili kwa wengine na atamtendea ubaya jirani yake"

walioshushwa

"watu ambao hawana heshima" au "watu ambao hakuna mtu anayewashimu"

waliotukuka

"watu wenye heshima" au "watu ambao kila mtu anawaheshimu"

Isaiah 3:6

na uharibifu huu uwe mikononi mwako

Hapa "mikono" inawakilisha mamlaka. "chukua usimamizi wa uharibifu huu" au "tawala juu ya uharibifu huu"

uharibifu huu

Maana zaweza kuwa 1) majengo mengi katika mji wa Yerusalemu yaliangamizwa au 2) watu katika Yerusalemu hawana mafanikio tena au uongozi. "mji huu, ambao sasa umeharibiwa"

sitakuwa mponyaji

Kutatua matatizo ya watu inazungumziwa kana kwamba ilikuwa kuwaponya. "Hapana, siwezi kutengeneza tatizo hili" au "Hapana, siwezii kukusaidia"

Isaiah 3:8

Kauli Kiunganishi

Nabii anaanza kutoa neno juu ya hii hali

Yerusalemu imejikwaa, na Yuda imeanguka

Kutomtii Mungu inazungumziwa kana kwamba ilikuwa ikijikwaa na kuanguka

macho ya utukufu wake

Hapa "macho" ina maana ya Mungu mwenyewe, ambaye ni mtukufu.

Mtazamo katika uso wao unashuhudia dhidi yao

Mionekano wa majiivuno katika nyuso za watu inazungumziwa kana kwamba mionekano ilikuwa watu ambao wanaweza kushuhudia dhidi ya watu wanaojivuna. "Mionekano ya kiburi juu ya nyuso zao zinaonyesha ya kwamba wanapingana na Yahwe"

wanasema juu ya dhambi yao kama Sodoma; hawaifichi

Hapa watu wa Yuda wanasemekana kuwa kama watu wa Sodoma, kwa sababu walijivuna wazi wazi kuhusu dhambi zao. "kama watu wa Sodoma, wanazungumza kuhusu dhambi zao na kuwaruhusu kila mtu ajue juu yao"

Kwa maana wamekamilisha maangamizi kwa ajili yao

Maangamizi bado yanakuja, lakini watu walimaliza kufanya kile kitakachosababisha kufuatia. Sababu za maangamizi zinazungumziwa kana kwamba zilikuwa ni balaa zenyewe. "Kwa maana wamefanya kila kitu ambacho kitasababisha maangamizi kutokea"

Isaiah 3:10

Mwambie mtu mwenye haki ya kwamba itakuwa ni salama

"Mwambie yule ambaye anafanya kilicho haki ya kwamba nitafanya mambo kuwa mazuri kwake"

mtu mwenye haki

Hii ina maana ya watu wenye haki kwa ujumla. "watu wenye haki"

kwa maana watakula matunda ya matendo yao

Matendo yazungumziwa kana kwamba yalikuwa miti itoayo matunda yanayoweza kuliwa. Tunda ina maana ya dhawabu ya kufanya matendo mema. "kwa maana watapokea dhawabu yao kwa ajili ya matendo yao mazuri" au "kwa maana watapokea dhawabu yao kwa ajili ya mambo mazuri waliyofanya"

watakula matunda ya matendo yao

Maandishi ya Kiebrania yana wingi wa kiwakilishi nomino hapa, lakini yana maana ya mtu mwenye haki yeyote. Watafsiri wanaweza kuchagua kutafsiri katika umoja. "atakula tunda la matendo yake"

kwa maana fidia ya mikono yake itafanyika kwake

Hapa "mikono" ina maana ya matendo ambayo mtu amefanya. "kwa kile ambacho mtu mwovu amefanya kwa wengine itafanyika kwake"

Watu wangu ... watu wangu

Maana zaweza kuwa 1) Isaya anazungumza na "wangu" kumaanisha Isaya, au 2) Yahwe anazungumza na "wangu" kumaanisha Yahwe.

watoto ndio wakandamizaji wao

Maana zawvza kuwa 1) "watu wachanga wamekuwa viongozi wao na wanakandamiza watu" au 2) "viongozi wao hawajakomaa kama watoto na wanakandamiza watu"

wanawake wanatawala juu yao

Maana zaweza kuwa 1) "wanawake wanatawala juu ya watu" au 2) "viongozi wao ni wadhaifu kama wanawake"

wale wanaokuongoza wanakuongoza nje ya mstari na kuchanganya muelekeo wa njia yako

Ilikuwa kawaida katika Mashariki ya Kati ya Zamani kuzungumza juu ya viongozi wa taifa kana kwamba walikuwa wachungaji. Mchungaji huongoza kondoo katika njia nzuri katika usalama, viongozi wanapaswa kuwafunza watu ukweli na kuwasaidia kufanya kilicho sahihi. Viongozi wa Yuda hawakuwa wakifanya hivi. "viongozi wako ni kama wachungaji wabaya na hawakuonyeshi mahali pa kwenda"

Isaiah 3:13

Yahwe husimama kwa ajili ya mashtaka; anasimama kuwashtaki watu

Isaya anazungumzia uamuzi wa Yahwe kudhuru watu kana kwamba Yahwe alikuwa akileta mashtaka halali katika mahakama dhidi ya watu wa Israeli. Sehemu ya pili ya mstari huu una maana hiyo hiyo na sehemu ya kwanza, lakini inasema kikamilifu zaidi. "ni kana kwamba Yahwe amechukua nafasi yake katika mahakama na alikuwa tayari kushtaki watu"

atakuja na hukumu

Hukumu inazungumziwa kana kwamba ilikuwa ni kitu ambacho mtu anawez kuleta kwa mtu mwingine. "atatangaza hukumu yake" au "atatamka hukumu yake"

Umeharibu shamba la mizabibu

Hapa "umeharibu" ina maana ya wazee na watawala. Yahwe anazungumzia juu ya watu wake kana kwamba walikuwa shamba la mizabibu. Kama mtu anayeshindwa kutunza shamba la mizabibu ili kwamba mizabibu zishindwe kuzaa matunda, wazee na viongozi wanakatisha tamaa Waisraeli kutomtumikia Mungu. "Watu wangu ni kama shamba la mizabibu, na umeliharibu"

Uporaji kutoka kwa maskini upo katika nyumba zenu

"vitu ulivyochukua kutoka kwa maskini zipo ndani ya nyumba zenu"

maskini

Kivumishi kidogo hiki kinaweza kuwekwa kama kivumishi. "wale ambao ni maskini"

Kwa nini unaponda watu wangu na kusaga nyuso za maskini?

Yahwe anauliza swali hili ili kwamba awashataki viongozi wa watu. Mashtaka haya yanaweza kuelezwa kama kauli. "Nina hasira na nyie watu waovu kwa sababu mnaponda watu wangu na kusaga nyuso za maskini"

unaponda watu wangu

Kufanya watu wangu kuteseka inazungumziwa kana kwamba ilikuwa kuwaponda na uzito mkubwa sana. "kuwaumiza watu wangu kwa ukatili"

kusaga nyuso za maskini

Kuwafanya watu kuteseka inazungumziwa kana kwamba ilikuwa kufuta nyuso zao katika ardhi. "kudhuru maskini na kuwafanya wateseke"

Isaiah 3:16

binti wa Sayuni

Sayuni, ina maana hapa mji wa Yerusalemu, anazungumzia kana kwamba ilikuwa mwanamke na binti zake. "wanawake wa Sayuni"

na vichwa vyao vikiwa juu

Hii ina maana kwa namna ya majivuno.

onyesha mapenzi kwa macho yao

Hapa "macho yao" yanawakilisha jinsi wanawaka wanavyowatazama. "wakijaribu kuwafurahisha wanamume kwa namna wanavyowatazama"

kutembea kwa maringo huku wakienda

"kuchukua hatua ndogo sana wanapotembea"

na kutoa mlio kama njuga kwa miguu yao

"kwa hiyo bangili katika vifundo vya miguu yao" au "kwa hiyo kengele katika vifundo vya miguu yao zilipiga kelele"

Isaiah 3:18

Taarifa ya Jumla

Hii inaendelea kumfafanua jinsi Yahwe atakavyohukumu wanawake wa Yerusalemu.

Bwana ataondoa

Hapa "ataondoa" inawakilisha kusababisha wengine kuondoa kitu. "Bwana atasababisha wengine kuondoa"

mapambo ya vito vya kifundo cha mguu

Pambo ambalo wanawake huvaa katika kifundo cha miguu, juu kidogo ya mguu.

ukanda wa kichwani

Pambo ambalo wanawake huvaa juu ya vichwa na nywele

mapambo yenye umbo la mwezi mwandamo

Mapambo yenye umbo la mwezi ambao watu huvaa kwa imani ya kwamba yatamlinda mtu kutoka na uovu.

lozi ya kidani ya sikioni

mapambo ya vito ambayo huning'inia kutoka kwenye sikio au juu ya sikio

bangili

Pambo ambalo wanawake huvaa katika mikono

shela

nyenzo nyembamba sana inayotumika kufunika kichwa na uso wa mwanamke

hijabu

vipande vyembamba vya nguo, virefu ambavyo wanawake hujifunga kuzunguka kichwa au nywele.

mkufu wa kifundo cha mguu

Haya ni mapambo ambayo wanawake huvaa karibu na miguu. Mara kwa mara mikufu huning'inia chini na kutoa sauti ya chini.

mishipi

kipande cha nguo ambacho watu huvaa kuzunguka kiuno au kupita kifuani.

visanduku vya manukato

kisanduku kidogo au mfuko unaokuwa na manukato ambayo wanawake walivaa juu ya mikufu au kamba kuzunguka shingo zao ili watoe harufu nzuri.

hirizi ya bahati

mapambo ya vito ambayo watu huvaa kwa imani ya kwamba italeta bahati nzuri

Isaiah 3:21

pete

pambo ambalo huvaliwa kuzunguka kidole

mapambo ya vito ya puani

pambo ambalo huvaliwa ndani ya au katika pua

joho la sikukuu

vazi refu linalolegea lenye mapambo ambalo lilivaliwa juu ya nguo zingine kwa kila mtu kuona

majoho

nguo inayovaliwa juu ya mabega kwa nje ya nguo

shela

nyenzo nyembamba sana inayotumika kufunika kichwa na uso wa mwanamke

mifuko ya mikononi

mfuko uliotumika kubeba vitu vidogo vidogo

vioo vya mkononi

uso mdogo, unaobebwa mkononi na kutumika kujitazama mwenyewe

kitani safi

kitambaa laini kinachovaliwa na watu matajiri

vipande vya kichwani

kitambaa au kofia ndogo inayovaliwa juu ya nywele

vifungashio

pambo la nguo ambalo mwanamke hujiviringishia kujifanya awe mzuri

Isaiah 3:24

mshipi

kipande cha nguo ambacho watu huvaa kuzunguka kiuno au kupita kifuani.

kamba

Hii inaweza kumaanisha kamba ambayo maadui wangefunga watu wa Yuda pale walipowakamata. Au inaweza kumaanisha ya kwamba wanawake wa Yerusalemu wangekuwa hawana kitu cha kuvaa ila nguo zilizochafuka zilizoshikwa kwa kamba.

nywele iliyopangwa vizuri, upaa

nywele zilizopangwa, upaa - "nywele nzuri, vichwa vyao vitakuwa na upaa"

Wanamume wenu wataanguka kwa upanga, na wanamume wenu wenye nguvu wataanguka vitani

Kuanguka ina maana ya kuuawa, na upanga inawakilisha vita. "Wanamume wenu watauawa vitani, na wanamume wenu wenye nguvu watauawa katika vita" au "Maadui wako watawaua wanajeshi wako katika vita"

malango ya Yerusalemu yataomboleza na kulia

Isaya anazungumzia malango ya mji kulia kana kwamba yalikuwa watu kama mfano wa maneno kwa ajili ya watu ambao watalia katika maeneo ya wazi karibu na malango. "Watu wa Yerusalemu watakaa katika malango ya mji na kulia na kuomboleza"

atakuwa peke yake na atakaa juu y ardhi

UIsaya anazungumzia watu wa Yerusalemu, ambao hakuna mtu atakayewaokoa kutoka kwa adui zao, kana kwamba walikuwa mji wao wenyewe na kana kwamba walikuwa mwanamke ambaye hukaa juu ya ardhi kwa sababu marafiki zake wote wamemuacha"

Isaiah 4

Isaiah 4:1

turuhusu tuchukue jina lako

Msemo huu una maana ya "turuhusu tukuoe"

tawi la Yahwe litakuwa zuri

Maana zawezekana kuwa 1) "tawi" ni neno lenye maana sawa na neno linalowakilisha mazao ambayo Yahwe atasababisha kuota katika nchi ya Israeli. "Yahwe atasababisha mazao katika Israeli kuwa mazuriu" au 2) "tawi" ni sitiari ambayo ina maana ya Masihi.

litakuwa zuri na lenye utukufu

"litakuwa limejaa uzuri na utukufu"

matunda ya nchi yakuwa matamu na ya kupendeza sana kwa wale waliosalia Israeli

"Matunda" mara kwa mara inawakilisha chakula kinachozalishwa katika nchiu, na mara nyingi inawakilisha baraka za kiroho. Maana hapa zawezekana kuwa 1) Mungu atasababisha nchi kutoa chakula kizuri tena. "watu ambao bado wapo Israeli watafurahia chakula bora kutoka katika nchi" au 2) Masihi ajaye ataleta baraka za kiroho kwa watu katika nchi.

Isaiah 4:3

yule ambaye amebaki Sayuni na yule ambaye anabaki Yerusalemu

Kauli hizi mbili zina maana moja. Hapa "yule ambaye" haimaanishi mtu dhahiri lakini watu kwa ujumla ambao bado wako hai Yerusalemu. "kila mtu ambaye anabaki Yerusalemu"

ataitwa mtakatifu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Bwana atawaita watakatifu" au "watakuwa wa Bwana"

kila mmoja ambaye ameandikwa chini kama aishiye Yerusalemu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "kila mmoja ambaye jina lake lipo katika orodha ya watu ambao wanaishi Yerusalemu"

Bwana atakapokuwa ameosha uchafu wa binti wa Sayuni

Msemo huu unazungumzia dhambi kana kwamba ilikuwa uchafu halisi. "baada ya Bwana kuondoa dhambiu ya binti wa Sayuni kama vile mtu anavyoosha uchafu"

binti wa Sayuni

Maana zawezekana kuwa 1) wanawake wa Yerusalemu au 2) watu wa Yerusalemu

na atakuwa amesafisha madoa ya damu kutoka miongoni mwa Yerusalemu

"Madoa ya damu" hapa yanawakilisha vurugu na mauaji. "na atakuwa amewaondoa wale walioko Yerusalemu ambao huwadhuru watu wasio na hatia"

kwa njia ya roho wa hukumu na roho anayewaka moto

Hii ni jinsi Mungu atakavyotoa dhambi kutoka Yerusalemu. Hapa "roho" huenda inawakilisha tukio la kuhukumu na kuchoma. "kwa hukumu na moto unaowaka"

roho wa hukumu

Maana zawezekana kuwa 1) Yahwe atawaadhibu watu au 2) Yahwe atawatangaza kuwa na hatia

roho awa moto uwakao

Maana zawezekana kuwa 1) hii ni sitiari ambayo inamaanisha Yahwe ataondoa wenye dhambi kutoka Sayuni kama moto uondoavyo uchafu au 2) "moto unaowaka" ni mfano wa maneno yanayowakilisha uharibifu kwa ujumla wa wenye dhambi wote.

Isaiah 4:5

kivuli juu ya utukufu wote

Maana zaweza kuwa 1) kivuli cha kulinda mji mtukufu, au 2) kivuli kinachojumuiusha utukufu wa Mungu ambao utalinda mji. Kama maana ya kwanza inafuata, basi inaweza kumaanisha zaidi ya kwamba mji ni tukufu kwa sababu Yahwe yupo mudo huo ndani yake.

kivuli

Hiki ni kitambaa ambacho huning'inizwa juu ya kitu kukifunika kwa ajili ya ulinzi.

Isaiah 5

Isaiah 5:1

Taarifa ya Jumla

Isaya anasema fumbo juu ya mkulima na shamba lake la mizabibu. Mkulima anawakilisha Mungu na shamba la mizabibu linawakilisha watu wa Yuda, ufalme wa kusini wa Waisraeli.

ninayempenda

"rafiki yangu kipenzi"

juu ya kilima chenye rutuba

"juu ya kilima ambapo mazao mazuri yanaweza kuota"

akachimbua kwa sepeto

"Ameandaa udongo". Msemo huu una maana ya kutumia kifaa kuchimba katika ardhi kuiandaa kwa ajilii ya kupanda.

Akajenga mnara katikati yake

"Alitengeneza jengo refu katikati ya shamba la mizabibu kuutazama". Mtu alikuwa akisimama juu ya mnara kutazama shamba la mizabibu na kuhakikisha hakuna wanyama au watu watakaoingia ndani mwake. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi.

kujenga kishinikizo cha zabibu

"alichimba shimo kuminya juisi ya zabibu". Kishinikizo cha zabibu ni sehemu ya chini iliyochongwa kwa jiwe katika ardhi ambapo wafanyakazi hukanyaga juu ya zabibu kuisaga kwa miguu yao, ili kutoa juisi ya zabibu.

zabibu mwitu

"zabibu zisizo na thamani" au "zabibu zenye ladha mbaya"

Isaiah 5:3

Taarifa ya Jumla

Katika fumbo la Isaya ya shamba la mizabibu, mmiliki wa shamba la mizabibu, ambaye anawakilisha Mungu, inazungumzia watu wa Yerusalemu na Yuda juu ya shamba lake la mizabibu.

wakazi wa Yerusalemu na mtu wa Yuda

Misemo hii ina maana ya ujumla watu wote wanaoishi Yerusalemu na Yuda, kwa hiyo iinaweza kutafsiriwa na nomino za wingi. "nyie wote ambao mnaishi Yerusalemu na Yuda"

Yerusalemu ... Yuda

"Yuda" ilikuwa jina la ufalme wa kusini wa Waisraeli, na Yerusalemu ulikuwa mji mkuu.

amua kati yangu na shamba langu la mizabibu

Wazo la nafasiii kugawanyisha vitu viwili mara kwa mara lilitumiika kueleza wazo la kuchagua moja kati ya nyingine ya vitu hivyo. "amua ni nani ametenda sahihi, mimi au shamba langu la mizabibu"

Ni kipi zaidi ambacho kingeweza kufanywa kwa ajili ya shamba langu la miiizabibu, ambalo sijafanya kwa ajili yake?

Mmilikii anatumia swali hili kutoa kauli juu ya shamba lake la mizabibu. Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Nimefanya kila nachoweza kwa ajili ya shamba langu la mizabibu"

Nilipoitazama kuzaa zabibu, kwa nini ilizaa mizabibu mwtu?

Mmiliki anatumia swali kusema ya kwamba shamba lake la mizabibu limezaa zabibu nzuri. Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Nilitaka kutengeneza zabibu nzuri, lakini ilizaa zabibu zisizo na thamani"

Isaiah 5:5

Taarifa ya Jumla

Katika fumbo hili, mmiliki wa shamba la mizabibu anaendelea kuzungumza juu ya shamba lake la mizabibu.

ondoa kitalu

"ondoa mpaka wa vichaka". Kitalu ni safu ya vichaka au miti midogo ambayo ilipandwa ili kulinda bustani au eneo lingine lolote. Hapa "kitalu" huenda ina maana ya vichaka vya miiba ambavyo vilipandwa kuota katika ukuta wa mawe unaozunguka shamba la mizabibu.

nitaibadili kuwa malisho

"nitaruhusu wanyama kwenda pale na kula". Hili ni eneo lenye nyasi ambapo wanyama hula.

itakanyagwa chini

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "wanyama watapakanyaga chini"

nitailaza kuwa takataka

"nitapaangamiza"

haitapogolewa wala kupaliliwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "hakuna mtu atapapunguza au kupapalilia" au "hakuna mtu atapakata matawi ambayo hayahitajiki, na hakuna mtu wa kutunza udongo"

mbigili na miiba itachipua juu

Mbigili na miiba mara kwa mara hutumika kama alama za miji na nchi zilizoharibiwa.

Isaiah 5:7

Taarifa ya Jumla

Isaya anafafanua fumbo la shamba la mizabibu.

Kwa ajili ya shamba la mizabibu la Yahwe wa majeshi ndiyo nyumba ya Israeli

"Kwa maana shamba la mizabibu la Yahwe wa majeshi linawakilisha nyumba ya Israeli" au "Watu wa Israelii ni kama shamba la mizabibu la Yahwe, Bwana wa majeshi ya malaika"

nyumba ya Israeli

Mataifa na makundi ya kikabila yanazungumziwa mara kwa mara katika Biblia kana kwamba yalikuwa nyumba, yaani, familia. "watu wa Israeli"

mtu wa Yuda mmea wake wa kufurahisha

"watu wa Yuda ni kama shamba la mizabibu ambalo huwapa watu starehe"

mtu wa Yuda

Hapa "mtu" inawakilisha watu wote wa Yuda. "watu wa Yuda"

alisubiri kwa ajili ya haki, lakini badala yake, kukawa na mauaji

Hii inaweza kubadilishwa ili kwamba nomino dhahania "haki" iweze kuelezwa kwa kitenzi "fanya kilicho haki". Nomino dhahania "mauaji" iuanweza kuelezwa kama "walijiua wao kwa wao". Yahwe alisubir watu kufanya kilicho haki, lakini badala yake walijiua wao kwa wao"

kwa ajili ya haki

Msemo "alisubiri" umeachwa lakini unaeleweka. Taarifa hii inayoeleweka inaweza kufanya maana kuwa wazi. "Alisubiri kwa ajili ya haki" au "Alisubiri kwa ajili yao kufanya kilicho haki"

badala yake, kelele za msaada

"badala yake, kulikuwa na kelele za msaada". Sababu ya watu kupiga kelele ya msaada inaweza kuwekwa wazi. "badala yake, wale ambao walikuwa dhaifu walipiga kelele kwa mtu kuwasaidia kwa sababu wengine walikuwa wakiwashambulia"

kelele

Msemo huu huenda una maana ya kelele nyingi.

Isaiah 5:8

Taarifa ya Jumla

Isaya anatangaza hukumu ya Mungu.

kwa wale ambao wanaunga nyumba kwa nyumba, ambao wanaunga shamba kwa shamba

"kwa wale ambao huchukua nyumba zaidi na zaidi, na yule ambaye huchukua mashamba zaidi na zaidi". Isaya anachukulia ya kwamba wasikilizaji wake wanajua ya kwamba sheria inakataza mtu kuchukua ardhi kutoka kwa familia kwa kudumu. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi.

Yahwe wa majeshi

Yahwe wa majeshi ya Israeli.

bila wakazi

"bila mtu yeyote anayeishi pale"

shamba la mizabibu la nira kumi

nira ya shamba la mizabibu Ukubwa wa shamba la mizabibu linawakilishwa na namba ya jozi za maksai ambao wanaweza kulilima katika siku moja. Kila jozi huunganishwa kwa nira. "shamba la mizabibu ambalo ni kubwa vya kutosha kwa jozi kumi za maksai kulilima"

bathi moja

"bathi moja ya divai" au "lita 22 ya divai"

homeri moja ya mbegu itatoa efa moja tu

"lita 220 za mbegu ztazaa lita 22 tu za nafaka". Homeri moja ni sawa na efa kumi.

Isaiah 5:11

wale ambao huamka mapema alfajiri ... ambao hukawia usiku kwa kuchelewa

Hii ina maana ya watu ambao hawafanyi lolote siku nzima lakini hunywa vinywaji vya kulewa.

mpaka divai inapowachoma

Hapa nguvu ya mvinyo kuwafanya wanywaji wake kulewa inazungumziwa kana kwamba ilikuwa ikiwachoma, yaani, kuwawasha moto. "hadi walewe kwa mvinyo"

kinubi, zeze, tari, filimbi na mvinyo

Hivi vyombo vya muziki na mvinyo zinaonyesha ya kwamba watu wanaofurahia vitu hivi wanasherehekea sana.

tari

Chombo cha muziki chenye kichwa kama ngoma ambacho kinaweza kupigwa kwa mkono. Huenda kilikuwa na vipande vya chuma vikizunguka upande ambao ilitoa sauti mpigaji alipokitikisa. Tari ilikuwa kidogo kwa mpigaji kukishika na kukitikisa kwa mkono mmoja.

kufikiria

"walifikiri kwa uzito juu ya"

matendo ya mikono yake

Hii inaweza kuandikwa tena ili kwamba nomino dhahania "matendo" yaelezwe kama kitenzi "kufanya" au "kuunda". "Kile alichofanya" au "kile alichounda"

matendo ya mikono yake

Hapa mifano ya maneno "mikono" inawakilisha mtu ambaye amefanya kitu. "Kile Yahwe alichofanya"

Isaiah 5:13

Taarifa ya Jumla

Mistari hii inasema kile kitakachotokea kwa watu kwa sababu hawajamtii Mungu.

watu wangu wamekwenda katika kifungo

Katika unabii vitu ambavyo vitatokea katika siku za usoni mara kwa mara vilimaanisha kana kwamba vilikwisha tendeka. Hii inasisitiza ya kwamba unabii utakuja kuwa kweli hakika. "maadui kutoka nchi zingine zitachukua watu wangu, Israeli, kama watumwa"

kwa ukosefu wa ufahamu

Kile ambacho hawaelewi inaweza kuwekwa wazi. "kwa sababu hawamuelewi Yahwe au sheria yake"

Kuzimu imefanya hamu yake kubwa zaidi na imefungua kinywa chake wazi sana

Msemo huu unazungumzia kuzimu, ambayo hapa ina maana ya kaburi, kwa mnyama ambaye yupo tayari kula wanyama wengine. Inasemekana ya kwamba watu wengi, wengi watakufa. "kifo ni kama mnyama mwenye njaa ambaye amefungua kinywa chake wazi kumeza watu wengi"

watu wao wenye uwezo, viongozi wao, na wale ambao wana furaha miongoni mwao, wanashuka kuzimu

Nabii anazungumzia kuhusu siku za usoni kana kwamba kinatokea sasa. "Watu wengi wa Israeli, watu wake muhimu na watu wa kawaida, viongozi wao na wale wanaofurahia sherehe, wataingia kuzimu"

Isaiah 5:15

Mtu atalazimishwa kuinama chini, na binadamu atashushwa

Misemo inayotumika pamoja ina mana moja na inatumika pamoja kwa msisitizo. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Mungu atafanya kila mtu kuinama chini na kuwa wanyenyekevu".

Mtu atalazimishwa kuinama chini, na binadamu atashushwa

Matukio ya siku za usoni yanazungumziwa kana kwamba vimekwisha tendeka.

Mtu atalazimishwa kuinama chini

Kuinama chini mara kwa mara inaashria kuaibishwa.

macho ya mwenye majivuno yatakuwa chini

Kuangalia chini mara nyingi ni ishara ya kuaibishwa. "macho ya watu wenye kiburi wataangalia chini kwa aibu" au "watu ambao wanamajivuno sasa wana aibu".

mwenye majivuno

Hapa watu wenye kiburi, majivuno wanazungumziwa kana kwamba wapo juu zaidi ya watu wengine. "kiburi"

Yahwe wa majeshi atainuliwa katika haki yake

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Watu watamsifu Yahwe wa majeshi kwa sababu ni mwenye haki"

Yahwe wa majeshi

Yahwe wa majeshi ya Israeli

atainuliwa

Kuheshimiwa inazungumziwa kana kwamba ni kuinuliwa juu. "ataheshimiwa sana"

kondoo watakula kama kwenye malisho yao wenyewe

Yahwe ataangamiza mji wa Yerusalemu, ambao uliitwa "shamba la mizabibu" katika 5:1. Litakuwa zuri bila chochote ila kwa ajili ya kondoo kula nyasi pale.

lisha

kula nyasi

katika uharibifu, kondoo watalisha kama wageni

Yaani, kondoo watalisha pale. Nchi itakuwa haina thamani kwa shughuli nyingine yoyote.

Isaiah 5:18

Ole wao ambao huvuta udhalimu kwa kamba zisizo na thamani na kuvuta dhambi kana kwamba iliikuwa kwa kamba ya mkokoteni

Misemo hii ina maana moja. Inazungumzia watu ambao wanaendelea kufanya dhambi kwa makusudi kana kwamba walikuwa wakitumia nguvu yao kuvuta mkokoteni mzito. Mungu atawaadhibu kwa ajili ya dhambi yao". "Ole wao ambao hufanya kazi kwa bidii kutenda dhambi kama mtu ambaye huvuta mkokoteni kwa kamba"

wale ambao husema

Hii ina maana ya wale ambao wanaendelea kutenda dhambi (mstari wa 18) na kisha kwa dhihaka kumpa na Mungu changamoto ya kuwazuia. "wale wadhihaki ambao husema"

acha mipango ya Mtakatifu wa Israeli aje

Mipango ya Mungu inazungumziwa kana kwamba ilikuwa vitu ambavyo vinaweza kuja vyenyewe. "acha Mtakatifu wa Israeli atimize mipango yake"

Mtakatifu wa Israeli

Mtakatifu wa Israeli

Isaiah 5:20

ambao huwakilisha giza kuwa nuru, na nuru kuwa giza ... uchungu kuwa utamu, na utamu kuwa uchungu

Wale wanaofanya vitu hivi ni sawa na wale ambao "huita uovu wema, na wema uovu". Vitu hivi ni kinyume na watu wanajua tofauti kati yao, lakini baadhi ya watu hudanganya na kusema mambo mabaya kuwa ni mema. "Wao ni kama watu ambao huita giza nuru na nuru giza. Wao ni kama watu wanaoita vitu vichungu vitamu na vitu vitamu vichungu"

kwa wale ambao wan hekima katika macho yao

Hapa mfano wa maneno "macho" una maana ya mawazo yao. "kwa wale ambao hujichukulia kuwa na hekima"

na wenye busara katika ufahamu wao

"na kufikiri wanaelewa kila kitu"

Isaiah 5:22

ambao huachilia waovu kwa malipo

Sehemu hii inasungumzia kuhusu hukumu iliyopotoshwa katika mahakama ya sheria.

huachilia waovu

"tamka wenye hatia kutokuwa na hatia"

hunyima asiye na hatia haki zake

"usiwatende watu wasio na hatia kwa haki"

Isaiah 5:24

ulimi wa moto

"mwale wa moto" au "mwale"

kama vile ulimi wa moto unavyomeza mashina ya mabua, na kama vile nyasi kavu zinavyoshuka chini katika mwale

Misemo hii ina maana moja. Mungu ataadhibu watu wanaoelezwa katika 5:18. "kama vile moto unavyochoma mashina ya mabua na nyasi"

mashina ya mabua

"mashina ya mazao yaliyokauka". Hii ina maana ya sehemu ya mmea ambao umebaki katika shamba kufa baada ya mkulima kukusanya chakula.

mzizi wao utaoza, na maua yao yatapulizwa mbali kama vumbi

Isaya anazungumzia watu hawa kana kwamba walikuwa mmea unaokufa. "watakufa kama mmea ambao mizizi yake imeoza na ambao maua yake yamekauka na kupulizwa katika upepo"

Isaiah 5:25

hasira ya Yahwe imewashwa

Isaya anazungumzia hasira ya Yahwe kana kwamba ilikuwa moto. "Yahwe ana hasira sana"

Amenyosha nje kwa mkono wake dhidi yao na amewaadhibu

Nabii anazungumza kuhusu siku za usoni kana kwamba imekwsha tokea. Anafanya hivi kusisitiza ya kwamba unabii utatokea kwa hakika. "atawaadhibu kwa mkono wake wenye nguvu"

amenyosha nje kwa mkono wake dhidi yao

Hapa "mkono" una maana ya nguvu ya Mungu na utawala. "ameonyesha nguvu yake dhidi yao"

mizoga

"miili iliyokufa"

mizoga yao ni kama takataka katika mitaa

Miili iliyokufa inaruhusiiwa kulala chini mitaani kana kwamba ilikuwa takataka. Hii inaonyesha ya kwamba wengi watakufa lakini hakuna mtu atakayekuwepo kuwazika. Neno "takataka" linaweza kutafsiriwa kama "iliyokataliwa" au "mbolea".

Katika haya yote, hasira yake haizimiki, badala yake, mkono wake

"Ingawa vitu hivi vyote vimetokea, bado ana hasira, na mkono wake"

mkono wake bado unanyoshwa nje

Hapa "mkono" unawakilisha nguvu na utawala wa Mungu. Isaya anazungumza kana kwamba Yahwe alikuwa mtu aliyekuwa tayari kumpiga mtu mwingine kwa ngumi yake. Hii ni sitiari kwa ajili ya Yahwe kuadhibu Israeli. "bado atakuwa tayari kuwaadhibu"

Isaiah 5:26

Atainua shara ya bendera kwa ajili ya mataifa ya mbali na atapiga mluzi kwa wale walio mwisho wa dunia

Isaya anasema jambo moja kwa njia mbili tofauti. Mungu kusababisha majeshi ya mataifa ambayo yapo mbali kutoka Yuda kuja na kushambulia inazungumziwa kana kwamba angeinua bendera na kupiga mluzui kuwaita kuja Yuda. "Atawaita majeshi ya mataifa ambayo yapo mbali kutoka Yuda na kuwaambia kuja"

piga mluzi

sauti ya juu ambayo mtu hufanya kwa mdomo wake kumuita mtu au mnyama ambaye yupo mbali.

watakuja

"jeshi la maadui litakuja"

kwa mbio na haraka sana

Maneno haya yana maana moja na yanasisitiza jinsi watavyokuja kwa haraka. "haraka sana"

Isaiah 5:27

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kufafanua jeshi ambalo litashambulia Yuda. Anafafanua kana kwamba tayai lilikuwepo.

huchoka ... huanguka ... husinzia ... hulala

Maneno haya manne yanaendelea kutoka kwenye kuchoka na kazi kwenda kutoweza kutembea vizuri, kwenda kutoweza kubaki macho, hadi kulala kabisa, kwa hiyo yote manne hutokea katika tafsiri.

Wala mikanda yao haijalegea

Wanajeshi waliweka nguo zao hali ya kubana ili iwe rahisi kusogea na kupigana.

mikanda ya ndara zao

"mikanda ya ndara zao"

kwato za farasi wao ni kama jiwe gumu

"kwato zao ni kama jiwe gumu". Isaya analinganisha sehemu ngumu ya mguu wa farasi kwa jiwe gumu, ambalo linaweza kusababisha cheche linapopigwa. Maana zaweza kuwa 1) Isaya analinganisha kwako zao ili kufafanua picha ya kutisha ya miguu yao kusababisha cheche wanapokimbia au 2) Isaya analinganisha kwato kwa jiwe gumu kusisitiza jinsi kwato zao ziilivyo na nguvu na zinavyomuwezesha farasi kufanya chochote bwana wake anachotaka kufanya.

na magurudumu ya vibandawazi vyao ni kama dhoruba

Isaya analinganisha matairi ya kibandawazi na dhoruba ili kuonyesha ya kwamba wataangamiza kila kitu katika njia yao. "na magurudumu ya vibandawazi yatazunguka kama dhoruba ya upepo"

magurudumu ya kibandawazi

Magurudumu haya mara kwa mara yana upapa uliochongoka ulionganishwa kwao ambao hukata mtu yeyote ambaye atapita karibu yake.

Isaiah 5:29

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kufafanua jeshi ambalo litaishambulia Yuda.

Kunguruma kwao kutakuwa kama simba, wataunguruma kama simba wachanga

Misemo hii miwili ina maana moja. Isaya analinganisha jeshi la adui kwa simba kuonyesha jinsi sauti ya shambulio lao litasababisha watu wa Yuda kuwa na hofu sana. "Pale ambapo jeshi lao linapiga kelele katika vita watakuwa kama simba anayeunguruma"

simba wachanga

Umri mdogo ni mfano wa maneno kwa ajili ya nguvu. "simba wenye nguvu"

Wataunguruma na kukamata mawindo

Isaya analinganisha adui kuwaua watu wa Yuda kwa simba kuwaua wanyama dhaifu. Maana zaweza kuwa 1) simba hutoa sauti isiyo ya juu kama ngurumo kabla hawajashambulia, au 2) mwandishi anatumia maneno mawili kumaanisha jambo moja.

mawindo

wanyama ambao wanyama wengine hutaka kuwshika na kuwala

bila mtu kuwaokoa

"na hakuna mtu atakayeweza kuwaokoa"

wataunguruma ... bahari inavyounguruma

Haya ni maneno yale yale yanayotafsiri "unguruma" katika mstari wa 29. Tumia neno ya lugha yako kwa sauti ya mawimbi katika dhoruba au mvua kubwa.

hata nuru itafanywa giza kwa mawingu

Hapa giza linawakilisha mateso na maafa. Sitiari hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "mawingu meusi yatafunika kabisa nuru kutoka kwa jua"

Isaiah 6

Isaiah 6:1

alikuwa juu na kunyanyuliwa

Maneno "juu" na "kunyanyuliwa" yanasisitiza ya kwamba kiti cha enzi kilikuwa juu sana na juu ya kila kitu kukizunguka. Urefu wa kiti cha enzi unawakilisha jinsiu Bwana alivyo mkuu na mwenye nguvu.

ulijaza hekalu

"ulijaza kasri". Neno linalotumika kwa ajili ya hekalu hapa mara kwa mara linatumika kumaanisha kasri ya wafalme.

Juu yake palikuwa na maserafi

Neno "maserafi" ni wingi wa serafi. Hii ina maana Bwana alikuwa amekaa juu ya kiti cha enzi na maserafi walikuwa wamesimama au wakipaa karibu na Bwana tayari kumtumikia.

maserafi

Neno hili linaashiria ya kwamba viumbe hawa wanaweza kuwa na muonekano wa ukali au kufanana na nyoka. Kwa sababu hatujui haswa nini "maserafi" inamaanisha, unaweza kutafsiri hili kama "viumbe wa mabawa" au "vitu vyenye uhai vyenye mabawa". Au unaweza kuazima neno na kutumia katika lugha yako.

kila mmoja wao alikuwa na mabawa sita

"kila serafi alikuwa na mabawa sita" au "kila kiumbe alikuwa na mabawa sita"

na mawili kila moja likifunika uso wake, na mawili yakifunika miguu yake, na mawili alipaa

Maneno "mabawa" na "serafi" yanaeleweka. "kwa mabawa mawili kila serafi alifunika uso wake, na kwa mabawa mawili alifunika miguu yake, na kwa mabawa mawili alipaa"

Isaiah 6:3

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kuelezea maono yake.

Kila mmoja alisema kwa mwingine na kusema

"Serafi aliita kwa mwingine na kusema" au "viumbe wenye mabawa walitamka kwa mwingine"

Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu, ni Yahwe wa majeshi

Kurudia neno "mtakatifu" mara tatu inaashiria Mungu ni mtakatifu kikamilifu. "Yahwe wa majeshi ni mtakatifu kuzidi kla kitu" au "Yahwe wa majeshi ni mtakatifu kabisa"

Dunia nzima imejaa utukufu wake

Hii inazungumzia dunia kana kwamba ilikuwa chombo na utukufu ulikuwa ujazo katika chombo. "Kila kitu juu ya dunia ni ushahidi wa utukufu wa Mungu"

Isaiah 6:4

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kufafanua maono yake.

Misingi ya vizingiti ilitetemeka kwa sauti ya wale waliokuwa wakilia kwa sauti

"Pale ambapo maserafi walitoa sauti, sauti zao zilitetemesha milango na misingi yao"

na nyumba ilijaa na moshi

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "na moshi ulijaza hekalu" au "na moshi ulijaza kasri"

Ole wangu! Maana nimeangamia

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Nipo katika matatizo makubwa! Mambo mabaya yatatokea kwangu"

wenye midomo michafu

Hapa "midomo" inawakilisha kile ambacho mtu anazungumza. Na, watu kusema mambo ambayo hayakubaliki kwa Mungu inazungumziwa kana kwamba midomo yao ilikuwa michafu kimwili.

Yahwe, Yahwe wa majeshi

Yahwe, mtawala wa jeshi la malaika

macho yangu yameona

Hapa "macho" yanawakilisha mtu mzima. "Nimeona"

Isaiah 6:6

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kufafanua maono yake.

maserafi

Neno hili linadokeza ya kwamba viumbe vinaweza kuwa na muonekano wa kutisha au kufanana na nyoka. Kwa sababu hatujui haswa nini "maserafi" ina maana gani, unaweza kutafsiri haya kama "viumbe" au "vitu hai" au "kiumbe". Au unaweza kuazima neno na kutumia katika lugha yako.

koleo

chombo kinachotumika kushika au kunyakua vitu

hatia yako imeondolewa, na dhambi yako imelipiwa

Misemo hii miwili kimsingi inasema kitu kimoja. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. Yahwe ameondoa hatia yako na amesamehe dhambi zako"

hatia yako imeondolewa

Yahwe kutomchukulii tena mtu kuwa na hatia inazungumziwa kana kwamba "hatia" ilikuwa kitu ambacho mtu anaweza kuondoa kutoka kwa mtu mwingine.

Isaiah 6:8

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kufafanua ono lake.

sauti ya Bwana inasema

Hapa "sauti" inawakilisha Bwana mwenyewe. "Bwana anasema"

nimtume nani

Inadokezwa ya kwamba Yahwe atamtuma mtu kuzungumza ujumbe wake kwa watu wa Israeli. "Nani nitamtuma kuwa mjumbe kwa watu wangu"

nani ataenda kwa ajili yetu

Inaonekana "yetu" ina maana ya Yahwe na washiriki wa baraza lake la mbinguni.

watu hawa

"watu wa Israeli"

Sikilizeni, lakini msielewe; tazameni, lakini msitambue

Maana zawezekana kuwa 1) vitenzi vya kuamuru "msielewe" na "mstambue" vinaeleza kile Mungu anasababisha kufanyika. "Utasikia, lakini Yahwe hatakuruhusu uelewe; utatazama kwa makini, lakini Yahwe hataruhusu uelewe" au 2) vitenzi vya kuamuru "Sikiliza" na "tazama" zinaeleza wazo la "kama". "Hata kama ukisikiliza hautaelewa; hata kama utatazama kwa makini, hautaelewa"

Sikilizeni, lakini msielewe; tazameni, lakini msitambue

Unaweza kueleza taarifa inayoeleweka kwa uwazi. "Sikiliza ujumbe wa Yahwe, lakini usielewe maana yake; tazama kile Yahwe anachofanya, lakini usigundue maana yake"

Isaiah 6:10

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kumwambia Isaya anachotakiwa kufanya pale ambapo Yahwe atamtuma kuhubiri kwa watu.

Fanya mioyo ya watu hawa kutokuhisi

Hapa "moyo" unawakilisha akili ya mtu. Mtu ambaye hafikiri kwa ufasaha na hawezi kuelewa na kujali juu ya kile kinachotokea inazungumziwa kana kwamba moyo wake hauna hisia. "Wafanye watu hawa kutoweza kuelewa" au "Fanya akili za watu hawa kufifia"

Fanya moyo wa watu hawa

Inaweza kuwa kawaida zaidi kutafsiri "moyo" na "hawa" kama wingi. "Fanya mioyo ya watu hawa"

Fanya moyo ... kutokuhisi

Amri hii ina maana ya kwamba Yahwe atatumia ujumbe wa Isaya kusababisha watu kuelewa kwa upungufu na kuwafanya kutojali kile Yahwe anachofanya.

masikio yao kufifia, na pofusha macho yao

"fanya ya kwamba wasiweza kusikia, na fanya ya kwamba wasiweze kuona". Isaya kufanya watu kutoelewa ujumbe wa Yahwe au kile anachofanya kinazungumziwa kana kwamba Isaya alikuwa akiwafanya kuwa viziwi na vipofu.

waweze kuona kwa macho yao, kusikia kwa masikio yao

Watu kuweza kuelewa ujumbe wa Yahwe na kile anachofanya inazungumziwa kana kwamba kama watu waliweza kuona na kusikia kimwili.

kuelewa kwa moyo wao

Hapa "moyo" unawakilisha akili ya mtu. Kuelewa kwa ukweli jambo na kujali juu ya kile kinachoendelea inazungumziwa kana kwamba watu walipaswa kuelewa kwa mioyo yao.

kisha kugeuka

Kutubu na kuanza kumtii Yahwe inazungumzwa kana kwamba watu waligeuka kwa Mungu kimwili. "mnifuate tena" au "kisha muanze kuniamini tena"

kuponywa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Ningewaponya"

Isaiah 6:11

Mpaka miji ianguke katika uharibifu na iwe bila wakazi, na nyumba iwe bila watu

"Mpaka miji yote na nyumba ziharibike na hakuna mtu anayeishi pale"

nchi huanguka katika takataka ya ukiwa

Hapa "huanguka katika" ni lahaja ambayo ina maana ya kuwa kitu kibaya zaidi. "nchi inakuwa takataka ya upweke"

Mpaka Yahwe awaondoe watu mbali, na upweke wa nchi ni mkubwa

Hapa Yahwe anazungumza kuhusu yeye mwenyewe katika mtu wa utatu. "Hadi mimi, Yahwe, nimewatuma watu wote mbali kabisa mwa nchi yao, ili kwamba hakuna mtu anayebaki"

Isaiah 6:13

itaangamizwa tena

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "majeshi yataangamiza nchi ya Israeli tena"

kama mvinje na mwaloni inapokatwa na mashina kubaki, mbegu takatifu ipo katika kisiki chake

Tashbihi hii ina maana ya kwamba hata baada ya Yahwe kuangamiza Israeli, atawatenga kando watu kutoka miongoni mwa Waisraeli kumtumikia.

mvinye

aina ya mti wa mwaloni

shina ... kisiki

Shina ni shina nene la mti. Kisiki ni sehemu ya mti ambayo inasalia kwenye ardhi baada ya mti kukatwa chini.

mbegu takatifu

Watu ambao watamtumikia Yahwe baada ya majeshi kuangamiza Israeli inazungumziwa kana kwamba walitengwa kando kama mbegu takatifu.

Isaiah 7

Isaiah 7:1

Katika siku za Ahazi ... mfalme wa Yuda

"Pale Ahazi... alipokuwa mfalme wa Yuda" Huu ulikuwa wakati matukio yalitokea.

Resini ... Peka ... Remalia

majina ya wanaume.

Resini ... na Peka ... alikwenda juu

Mwandishi anazungumza kana kwamba wafalme walikuwa majeshi walioyaongoza. "Resini ... na Peka ... waliongoza majeshi yao juu"

kufanya vita dhidi yake

Mwandishi anazungumza kana kwamba mji wenyewe ulikuwa watu ambao huishi ndani yake. "kupiga vita dhidi ya watu wa Yerusalemu"

Ikasemekana katika nyumba ya Daudi

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Nyumba ya Daudi ikasikia taarifa" au "mtu alitoa taarifa kwa nyumba ya Daudi"

nyumba ya Daudi

Neno "nyumba" ni mfano wa maneno kwa ajili ya familia inayoishi katika nyumba. "Mfalme Ahazi na washauri wake"

ya kwamba Aramu alishirikiana na Efraimu

Hapa "Aramu" na "Efraimu" wanatambua wafalme wao. Efraimu anatumiwa hapa kumaanisha ufalme mzima wa kaskazini wa Israeli. "ya kwamba Resini, mfalme wa Aramu alikuwa akimsaidia Peka, mfalme wa Israeli"

Moyo wake ulitetemeka, na moyo wa watu wake, kama miti ya msituni inavyotetemeka katika upepo

Kutetemeka kwa mioyo yao katika habari hii inalinganishwa na namna miti hutikisika pale upepo unapovuma katikati yao. "Ahazi na watu wake waliogopa sana"

Isaiah 7:3

Maelezo ya Jumla

Isaya anaandika juu ya kile kilichotokea kwake kana kwamba kilitokea kwa mtu mwingine.

Shear-yashubu

Watafsiri wanaweza kuongeza maandishi kwa chini ambayo yanasema, "Jina la Shear-yashubu ina maana ya 'waliobakia watarudi'". Maana inaweza kuwa imempatia matumaini Ahazi.

katika mwisho wa mfereji wa dimbwi la juu

"ambapo maji huingia katika dimbwi la juu"

mfereji

mtaro wa kutengenezwa na mtu au chini mwa chini mwa mlima ambmo maji hutiririka

barabara

barabara laini kama la lami.

shamba la dobi

Maana zaweza kuwa 1) hii ni jina la kufaa ambalo watu waliita shamba au 2) hii ni nomino ya kawaida ambayo watu walitumia kuongea juu y shamba, "shamba la dobi" au "shamba ambapo watu huosha sufu"

shamba la dobi

Dobi huwa ni 1) mwanamume ambaye hufua sufu ambayo mtu kanyoa katika kondoo, "Shamba la Mfuaji wa Sufu" au 2) mwanamke ambaye hufua nguo chafu, "Shamba la Mfuaji wa Nguo"

Mwambie

"Mwambie Ahazi"

usiogope au kutishwa kwa mikia ya moto miwili ya kichiniichini, kwa hasira kali ya Resini na Aram, na ya Peka mwana wa Remalia

Mungu analinganisha Resini na Peka kwa njiti zinazowaka ambao moto wake umezimika na kufanya moshi. Mungu anasisitiza ya kwamba sio vitisho vya kweli. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "usimruhusu Resini na Peka kukutisha; hasira yao katili ni kama kijiti kiwakacho ambacho moto wake umezimika na kuna moshi pekee"

usiogope au kutishwa

Maneno "ogopa" na "tishwa" yana moja na yanaweza kutafsiriwa kama neno moja.

Isaiah 7:5

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kumwambia Isaya kile anachotakiwa kumwambia Ahazi.

Aramu, Efraimu, na mwana wa Remalia

Maneno "Aram" na "Efraimu" yana maana ya wafalme wa nchi hizi. Pia, "Efraimu" ina maana ya ufalme wa kaskazini wa Israeli. "Resini mfalme wa Aramu na Peka mwana wa Remalia, mfalme wa Israeli"

Remalia

Hili ni jina la mwanamume.

wamepanga uovu dhidi yako

Hapa "yako" ni umoja na ina maana ya Ahazi.

mwana wa Tabeeli

Haijulikani mwanamume huyu ni nani.

Isaiah 7:7

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kumwambia Isaya kile anachotakiwa kumwambia Ahazi.

na mkuu wa Dameski ni Resini

"na mfalme wa Dameski ni Resini, ambaye ni mtu dhaifu"

miaka sitini na tano

miaka mitano "miaka 65"

Efraimu atavunjwavunjwa na hatakuwa kundi la watu tena

Hapa "Efraimu" ina maana wote wa ufalme wa kaskazini wa Israeli. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "jeshi litaangamiza Efraimu, na hapatakuwa tena na watu wa Israeli"

mkuu wa Samaria ni mwana wa Remalia

Hii ina maana Peka ni mfalme wa Samaria na Israeli yote. "mfalme wa Samaria ni Peka, ambaye n mwanamume dhaifu"

kama hautabaki imara katika imani, hakika hautabaki salama

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Ukiendelea kuamini ndani yangu, hakika utabaki salama"

kama hautabaki

"hadi ubaki"

Isaiah 7:10

iombe kwa kina au katika maref ya juu

Yahwe anatumia neno "kina" na "urefu" kumaanisha Ahazi anaweza kumuuliza jambo lolote.

kina ... marefu

Nomino dhahania "kina" na "urefu" inaweza kutafsiriwa kwa vihusishi. "sehemu mbali chini yako ... sehemu mbali juu yako"

sitaiomba

"sitamuomba Yahwe kwa ajili ya ishara"

Isaiah 7:13

nyumba ya Daudi

Neno "nyumba" ni mfano wa maneno kwa ajili ya familia nayoishi katika nyumba. "Mfalme Ahaz, wewe na washauri wako"

Je! haitoshi kwenu watu kujaribu uvumilivu wa watu? Je! ni lazima mjaribu uvumilivu wa Mungu wangu?

Maswali haya yanasisitza ya kwamba mflme ametenda dhambi sana. "Unajaribu uvumilivu wa watu! Sasa unajaribu uvumilivu wa Mungu wangu!"

mwanamke kijana atapata mimba

Baadhi ya tafsiri za zamani na tafsiri za kisasa hutafsiri, "bikira atapata mimba", huku zingine "mwanamke kijana atapata mimba"

jina lake Imanueli

Watafsiiri wanaweza kuongeza maandishi ambayo yanasema: "Jina Imanueli lina maana 'Mungu pamoja nasi'".

Atakula magandi na asali anapojua kukataa uovu na kuchagua mema

Maana zaweza kuwa 1) "Hadi kufikia muda huyo mtoto amekua vya kutosha kula magandi na asali, ataweza kukataa kilicho kiovu na kuchagua kilicho chema." Hii inasisitiza ya kwamba mtoto atakuwa mdogo sana atakapojua kuchagua kipi ni sahihi badala ya kibaya au 2) "Hadi kufikia muda mtoto amekua vya kutosha kukataa kilicho kiovu na kuchagua kilicho chema, atakuwa anakula magandi na asali". Watu wa Yuda walichukulia mtoto kuwajibika kwa kufanya mema aliipokuwa na umri wa miaka 12. Hii inasisitiza ya kwamba ndani ya miaka kumi na mbili watu wataweza kula magandi na asali kwa sababu watu wengi zaidi wa Israeli watauliwa au kuchukuliwa kama mateka.

magandi

maziwa ambayo watu wameyatengeneza kutengeneza kuwa ugumu laini

kukataa uovu na kuchagua mema

"kataa kufanya matendo maovu na chagua kufanya mambo mema"

Isaiah 7:16

Maelezo ya Jumla

Hii ina maana ya watu wa Yuda

kukataa uovu na kuchagua mema

"kataa kufanya matendo maovu na kuchagua kufanya mambo mema".

unaowahofia

"unaogopa". Hapa "unaowahofia" ni umoja na ina maana ya Ahazi.

watu wako

Hii ina maana ya watu wa Yuda.

Efraimu alijitoa kutoka kwa Yuda

"watu wa Efraimu kugawanya kutoka kwa watu wa Yuda"

Isaiah 7:18

Kwa kipindi hicho

kabla mtoto kujua kukataa uovu na kuchagua mema

Yahwe atapiga mluzi kwa

"Yahwe atawaita" au "Yahwe atawaita mahakamani"

kwa ajili ya inzi aliyeko katika vijito vya mbali vya Misri, na kwa ajilii ya nyuk kutoka nchi ya Ashuru

"kwa maana majeshi ya Misri na Ashuru, na wanajeshi wao yatakuwa kila sehemu kama inzi na nyuki"

Isaiah 7:20

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kufafanua kipindi ambacho jeshi la Ashuru litavamia Israeli.

Bwana atanyoa kwa wembe ambao ulikodiwa upande wa pili wa Mto Frati - mfalme wa Ashuru

Neno "wembe" ni sitiari kwa ajili ya mfalme wa Ashuru na jeshi lake, na Yahwe anazungumzia mfalme kana kwamba mfalme alikuwa mwanamume ambaye angefanya kazi ya Yahwe na kisha kupokea fedha kutoka kwa Yahwe. "Bwana atamuita mfalme wa Ashuru kutoka ng'ambo ya Mto Frati kufanya kazi kwa ajili yake kukunyoa"

ambao ulikodiwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "ambao alinunua"

kichwa ... nywele za miguuni ... pia ... ndevu

Ilikuwa vibaya kwa mtu kunyoa sehemu ya juu ya kichwa chake; ilikuwa vibaya zaidi kwa mtu kunyoa "nywele za miguu"; ilikuwa vibaya kuliko zote kwa mtu kunyoa ndevu.

kichwa ... nywele za miguuni ... ndevu

Isaya hasemi ni kichwa cha nani, nywele, na ndevu ambazo Bwana anakwenda kunyoa, lakini Ahazi na msomaji wataelewa ya kwamba huyu ni mwanamume; mwanamume ni sitiari kwa ajili ya watu wanaoishi katika nchi ya Yuda.

kichwa

"nywele katika kichwa"

nywele za miguuni

Maana zaweza kuwa 1) hii ni njia ya upole kuzungumza juu ya nywele katika sehemu ya chini ya mwili au 2) hii inazungumzia nywele katika miguu.

pia itafyeka

"wembe utafyeka pia". Iwapo lugha yako inahitaji mtu kuwa mhusika wa "atafyeka", unaweza kusema, "Bwana pia atafyeka".

kwa sababu y wingi wa maziwa ambayo watayatoa

Nomino dhahania "wingi" unaweza kutafsiriwa kama kishazi. "kwa sababu watatoa maziwa mengi sana"

Isaiah 7:23

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kufafanua kipindi ambacho jeshi kutoka Ashuru litashambulia nchi ya Israeli.

palipokuwa na mizabibu elfu moja ... mibigili na miiba

"kulikuwa na mizabibu 1,000". Yaani, Isaya alipoandika, kulikuwa na mashamba ya mizabibu, ambazo baadhi yao kulikuwa na mizabibu 1,000 au zaidi. Anasema ya kwamba mashamba haya ya mizabibu yatajaa mibigili na miiba"

shekeli elfu moja za fedha

"shekeli 1,000 za fedha". Shekeli ni sarafu ya fedha yenye thamani ya mshahara wa siku 4. "sarafu 1,000 za fedha"

mibigili na miibaa

Maneno "mibigili" na "miiba" yote ina maana ya kutokuwa na thamani, mimea ya miiba. "vichaka vya miiba" au "vichaka vya mibigili"

kwa sababu nchi yote itakuwa mibigili na miiba

Kwa nini wawindaji watakuja katika nchi hizi inaweza kuwekwa wazi. "kwa sababu hakutakuwa na kitu katika nchi hizi ila mibigili, miiba, na wanyama pori"

Watakaa mbali na vilima vyote ambavyo vililimwa kwa jembe

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Watu watakaa mbali na vilima ambamo hapo awali ziliandaa udongo kupanda mazao"

Isaiah 8

Isaiah 8:1

Yahwe alisema kwangu

Hapa neno "kwangu" ina maana ya Isaya.

Nitawaita kortini mashahidi waaminifu kushuhudia kwa ajili yangu

Maana zaweza kuwa 1) Yahwe anazungumza "Nitawaita watu waaminifu kuwa mashahidi" au 2) Isaya anazungumza: "Niliwaita wanamume waaminifu kuwa mashahidi" au 3) Yahwe anamuamuru Isaya: "Waite wanamume waaminifu kuwa mashahidi"

Isaiah 8:3

Nilikwenda kwa nabii wa kike

Inaweza kuwekwa wazi ya kwamba Isaya alimuoa nabii wa kike. "Nililala na mke wangu, nabii wa kike"

utajiri wa Dameski na nyara za Samaria zitachukuliwa na mfalme wa Ashuru

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "mfalme wa Ashuru atabeba hazina zote za Dameski na Samaria"

Isaiah 8:5

Kwa sababu watu hawa wamekataa maji ya pole pole ya Shiloa

Maneno "maji ya pole pole" ni sitiari kwa ajili ya sheria ya Mungu. "Kwa sababu watu hawa wamekataa sheria ya Yahwe, ambayo ni kama maji ya pole pole ya Shiloa"

watu hawa

"kundi hili la watu". "watu hawa wamekataa ... wana furaha"

na wana furaha juu Resini na mwana wa Remalia

Maana kamili inaweza kuwekwa wazi. "na wana furaha ya kwamba majeshi ya AShuru yameshinda Resini, mfalme wa Aramu, na Peka, mwana wa Remalia, mfalme wa Israeli.

kwa hiyo Bwana

Yahwe anazungumza juu yake kana kwmba alikuwa mtu mwingine kuwakumbusha watu yeye ni nani. "kwa hiyo, Mimi, Bwana, ni"

kuleta juu yao

Kitenzi ni "kuleta juu"; kielezi ni "juu yao".

juu yao

"ju ya watu wa Yuda"

maji ya Mto, yenye nguvu na mengi, mfalme wa Ashuru na utukufu wake wote

Mto unaashiria jeshi la Ashuru. "jeshi kutoka Ashuru, ambalo lina nguvu kama mto wenye nguvu"

Mto

Mto Frati katika Ashuru

Isaiah 8:8

Maelezo ya Jumla

Bwana anaendelea kufafanua jeshi la Ashuru kama mto ambao utafurika Yuda.

Mto utafagia mbele mpaka Yuda, kufurika na kupitiliza mbele, hadi ufike shingoni mwako

Jeshi la Ashuru ni kama maji yafurikayo. "Wanajeshi zaidi na zaidi watakuja kama mto unaopanda juu ya shingo yako"

Mto

Mto Frati katika Ashuru. Huu ni mfano wa maneno kwa ajili ya wanajeshi wa Ashuru, ambao watakuja kutoka katika nyumba zao kwa Mto Frati.

mabawa yake yaliyonywoshwa yatajaza

Maana zaweza kuwa 1) kama "Mto" kwa sitiari kuinua, "mabawa" yake kutiririka juu na kufunika kile kilichokuwa nchi kavu au 2) Isaya anabadili sitiari na sasa anazungumza juu ya Yahwe kama ndege anayelinda nchii, "Lakini mabawa yake yaliyonywoshwa yatafunika"

Imanueli

Watafsiri wanaweza kuongeza maandishi yanayosema: "Jina Imanueli lina maana ya 'Mungu pamoja nasi'"

Isaiah 8:9

Watu wako watavunjwa vipande vipande

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Nitavunja majeshi yako vipande vipande"

Sikiliza, nyie nchi za mbali

Isaya anazungumza kana kwamba watu katika nchi zingine wanaweza kumsikiliza. "Sikiliza, nyie watu wote mlio sehemu za mbali"

jiwekeni tayari kwa ajili ya vita na mvunjike vipande vipande; jiwekeni tayari na mvunjike vipande vipande

Hii ina maana ya jambo moja, inatajwa mara mbili kwa msisitizo. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "unaweza kujiandaa kwa ajili ya vita, lakini nitakushinda"

Unda mpango, lakini hautatekelezwa; toa amri, lakini haitatekelezwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Unaweza kujiandaa kushambulia Yuda, lakini hautafanikiwa"

haitatekelezwa ... haitatekelezwa

"Kutekeleza" mpango au amri ni kufanya kile ambacho mtu aliyefanya mpango au amr anataka msikilizaji afanye. Vishazi hivi vinaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "hautaweza kufanya kile unachopanga kufanya ... wanajeshi wako hawataweza kufanya kile makamanda wao wanawaambia kufanya"

Isaiah 8:11

Yahwe alizungumza kwangu, kwa mkono wake wa nguvu juu yangu

"Yahwe alizungumza kwangu kwa njia ya nguvu sana"

na kunionya nisitembee katika njia ya watu hawa

Hii ni nukuu isiyo moja kwa moja ambayo huisha katika 8:17. "na kunionya na kusema, 'Usitende kama watu hawa'"

Usiite njama kitu chochote ambacho watu hawa wanaitwa njama

Watu wanawaza kuna njama, na inawafanya wawe na wasiwasi. "Usiwe na wasiwasi kama watu ambao wanadhani mtu anajaribu kuwadhuru muda wote"

Ni Yahwe wa majeshi ambaye utamheshimu kama mtakatifu; yeye ndiye unayepaswa kumuogopa, na yeye ndiye unapaswa kumhofia

Kama utatafsiri hii kama nukuu ya moja kwa moja, pia unaweza kutafsiri na Yahwe kuzungumza katika mtu wa kwanza. "Lakini utanifikiria, Yahwe wa majeshi, kama mtakatifu. Na utaniogopa na kuwa na hofu kwangu"

Isaiah 8:14

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendeleza nukuu isiyo moja kwa moja ya Yahwe ambayo ilianza katika 8:11. Inaweza kutafsiriwa kama nukuu ya moja kwa moja na Yahwe akizungumza katika mtu wa kwanza.

Atakuwa mahali patakatifu

Neno "mahali patakatifu" ni sitiari kwa ajili ya Yahwe kuwaweka watu wake salama na kuwalinda. "Atawalinda watakapokwenda kwake"

atakuwa jiwe la kupiga, na mwamba wa kujikwaa

Maneno "jiwe la kupiga" na "mwamba wa kujikwaa" yote ni sitiari kwa ajili ya Yahwe kudhuru watu wake. Baadhi wanatafsiri "kupiga" na "kujikwaa" kama "kujikwaa" na "kuanguka"; wengine wanatafsiri kama "kosa" na "kujikwaa". "atawadhuru watu wake, kama mwamba ambao watu hupiga miguu yao na kujikwaa, na kama mwamba ambao husababisha watu kuanguka"

atakuwa mtego na kikwazo kwa watu wa Yerusalemu

Maneno "mtego" na "kikwazo" ina maana karibu na kitu kimoja na inasisitiza ya kwamba pale ambapo Yahwe ataamua kuadhibu watu wa Yerusalemu hawataweza kutoroka. "atawatega watu wa Yerusalemu ili wasiweze kumtoroka"

mtego

chombo ambacho hukamata ndege katika wavu au kikapu

kikwazo

mtego ambao hukamata na kushika mguu wa mnyama au pua

Wengi watajikwaa juu yake na kuanguka na kuvunjika, na kutegwa na kukamatwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Watu wengi watajikwaa ju ya jiwe, na watakapoanguka hawatainuka. Na watu wengi watakanyaga katika mtego, na hawataweza kutoka"

kutegwa na kukamatwa

Maneno haya mawili yana maana moja na yanasisitiza ya kwamba watashikwa katika mtego.

Isaiah 8:16

Ufunge ushuhuda wangu, wekea muhuri kumbukumbu halali

Misemo hii miwili ina maana moja. "Funga kwa nguvu hati ya kukunja kwa ujumbe huu ulioandikwa juu yake"

ushuhuda wangu ... wanafunzi wangu

Haipo wazi ni kwa nani neno "wangu" ina maanisha nini. Inaweza kuwa Isaya au Yahwe. Ni vyema kuacha kiwakilishi kuwa na maana nyingi.

Nitamsubiri Yahwe

Hapa "nitamsubiri" ina maana ya Isaya.

ambaye huficha uso wake kutoka katika nyumba ya Yakobo

"uso" wa Yahwe ni mfano wa maneno kwa ajili ya baraka au fadhila yake. "ambaye amechukua baraka yake kutoka katika nyumba ya Yakobo" au "ambaye hatazami kwa fadhila tena juu ya nyumba ya Yakobo"

nyumba ya Yakobo

watu wa Israeli

Mimi na wana ambao Yahwe amenipatia ni kwa ajili ya ishara na maajabu katika Israeli

"Mimi na wana ambao Yahwe amenipatia ni kama isihara kuwaonya watu wa Israeli". Wana ni Shear-yashubu na Maher-shalal-hash-bazi, ambao majina yao ni ujumbe kwa watu wa Israeli.

Isaiah 8:19

Maelezo ya Jumla

Isaya anazungumza

Watasema kwako, "Shauriana na watu wanaowasiliana na mizimu na wachawi", wale ambao hulia na nung'unika dua. Lakini watu wasitafute ushauri kwa Mungu wao? Je! watafute ushauri kwa wafu kwa niaba ya walio hai? Kwa sheria na kwa ushuhuda!

Maana zingine zaweza kuwa 1) "Watasema kwako, 'Watashauriana na wanaowasiliana na mizimu na wachawi, wale ambao hulia na ung'unika dua. Lakini watu wasitafute ushauri kwa Mungu wao? Je! watafute ushauri kwa wafu kwa niaba ya walio hai? Kwa sheria na kwa ushuhuda!'" au 2) "Watakaposema kwako, 'Watashauriana na wanaowasiliana na mizimu na wachawi, wale ambao hulia na ung'unika dua. Lakini watu wasitafute ushauri kwa Mungu wao? Je! watafute ushauri kwa wafu kwa niaba ya walio hai? Kwa sheria na kwa ushuhuda!

Watasema kwako

Neno "watasema" lina maana ya wale ambao humtumaini Yahwe. Neno "kwako" ni wingi na lina maana ya wale ambao wanamtumaini Yahwe.

Shauriana na watu wanaowasiliana na mizimu na wachawi

"Waulize wanaowasiliana na mizimu na wachawi unachpaswa kufanywa"

wanaowasiliana na mizimu na wachawi

wale ambao hudai kuzungumza na wale ambao wameshakufa

wale ambao hulia na nung'unika dua

Maneno "hulia" na "nung'unika" yana maana ya sauti ambazo wanaowasiliana na mizimu na wachawi hufanya wanapojaribu kuzungumza na wafu. "wale ambao hunong'oneza na kunung'una maneno yao ya kichawi kujaribu kuzungumza na watu waliokufa"

hulia

kufanya sauti kama ya ndege

Lakini watu wasitafute ushauri kwa Mungu wao? Je! watafute ushauri kwa wafu kwa niaba ya walio hai?

Maswali haya yanaonyesha ya kwamba watu wanaweza kushauriana na Mungu badala ya matendo yao ya kipumbavu ya kujaribu kuzungumza na watu waliokufa. "Lakini watu wanapaswa kumuuliza Yahwe kuwaongoza. Hawapaswi kutafuta majibu kutoka kwa wale waliokufa"

Kwa sheria na kwa ushuhuda!

Maana zaweza kuwa 1) "Kuwa makini na maelekezo ya Mungu na mafunzo" au 2) "Kisha unatakiwa kukumbuka mafundisho na ushuhuda niliokupatia"

sheria

Hili ni neno hilo hilo lililotafsiriwa "kumbukumbu halali" katika 8:16

ushuhuda

Inaweza kuwa Isaya au Yahwe. Ni vyema kuacha kiwakilishi kuwa na maana nyingi.

Iwapo hawatasema vitu hivi

"Kama hawatazungumza juu ya sheria na ushuhuda"

ni kwa sababu hawana nuru ya alfajiri

Isaya anazungumzia watu ambao hawamjui Mungu kana kwamba walikuwa watu wanaotembea katika giza bila mwanga wowote. "ni kwa sababu wao ni kama mtu aliyepotea gizani"

Isaiah 8:21

utusitusi wa kukandamiza

"huzuni mbaya"

Wataendeshwa katika nchi ya giza

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe atawaondoa nje katika giza kamili"

Isaiah 9

Isaiah 9:1

Huzuni itaondolewa kutoka kwake ambaye alikuwa katika maumivu makali

Isaya anazungumzia watu ambao wamepotea kiroho kana kwamba walikuwa wakitembea katika giza tupu. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe ataondoa giza kutoka kwake aliyekuwa katika maumivu makali"

Huzuni

Neno hili lina maana ya "giza kidogo au giza tupu".

kwake ambaye alikuwa katika maumivu makali

"yeye ambaye alikuwa akiteseka maumivu makali na huzuni". Huenda hii ni sitiari kwa ajili ya watu wa Yuda

Katika kipindi cha awali aliabisha nchi ya Zabulonii na nchi ya Naftali

"Nchi" ina maana ya watu ambao wanaishi katika eneo. "Kipindi cha nyuma, Bwana aliwashusha waleabuloni na Naftali"

lakini katika kipindi cha baadaye ataifanya iwe tukufu, njia ya baharini, mbele ya Yordani, Galilaya ya mataifa

Hapa "ataifanya" ina maana ya Galilaya ambayo inawakilisha watu wanaoishi kule. "lakini katika siku za usoni, Bwana ataheshimu watu wa Galilaya wa mataifa, ambayo ipo katika barabara kati ya Bahari ya Mediteranea na Mto Yordani"

Galilaya ya mataifa

Hapa "mataifa" yanawakilisha watu kutoka mataifa mengine ambao wanaishi Galilaya. "Galilaya, ambapo wageni wengi huishi"

waliotembea gizani ... walioishi katiika nchi ya kivuli cha kifo

isaya anazungumzia watu kuishi maisha ya dhambi na mateso kwa sababu yake kana kwamba walikuwa wakitembea katika nchi ya giza na yenye kivuli cha kifo.

mwanga mkubwa ... mwanga umewaka

Hapa "mwanga" unawakilisha matumaini na ukombozi.

nchi ya kivuli cha kifo

Msemo "kivuli cha kifo" ni lahaja ambayo ina maana ya giza nene. "nchi yenye giza zito"

Isaiah 9:3

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kuelezea kipindi ambapo Mungu atawaokoa watu wa Israeli. Ingawa matukio haya yatatokea katika siku za usoni (9:1), Isaya anayafafanua kana kwamba yamekwisha tokea. Hii inasisitiza ya kwamba yatatokea hakika.

Umezidisha taifa; umeongeza furaha yao

Neno "umezidisha" ina maana ya Yahwe. Neno "yao" ina maana ya watu wa Israeli, lakini Iisaya anajijumlisha kama sehemu ya Israeli. "Bwana, utaongeza sana watu wetu na furaha yetu"

Wanafurahi mbele yako kama furaha ya kipindi cha mavunno, kama wanamume wanavyofurahi wanapogawana nyara zao

"Watafurahi mbele yako kama watu wanavyofurahi wanapokusanya mazao yao au pale vita inakamilika na wanajeshi kugawanya kiile walichochukua"

Isaiah 9:4

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kufafanua kipindi ambacho Mungu ataokoa watu wa Israeli. Ingawa matukio haya yatatokea katika kipindi cha usoni. Isaya anayafafanua kana kwamba yalikuwa yametokea tayari. Hii inasisitiza ya kwamba hakika itatokea.

Kwa maana nira ya mzigo wake ... umeharibika kabisa kama katika siku ya Midiani

Isaya anazungumzia Waisraeli, ambao ni watumwa wa Ashuru, kana kwamba walikuwa ng'ombe anayevaa nira. Hii itatokea katika siku za usoni, lakini anazungumza kana kwamba tayari imetokea tayari. "Kwa maana kama katika siku ya Midiani utawaweka watu wa Israeli huru katika utumwa kwa wakandamizaji wao kama mtu anavyotoa nira kutoka mabegani mwa mnyama"

Kwa maana nira ya mzigo wake .... bega lake ... mkandamizaji wake

Isaya anazungumzia watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja. "Kwa maana nira ya mzigo wao ... mabegani mwao ... wakandamizaji wao"

mhimili katika bega lake

Mhimili ni sehemu ya nira ambayo huenda juu ya mabega ya ng'ombe

mhimili

Maana nyingine yaweza kuwa "gongo", kipande kirefu cha mbao ambacho mtu hutumia kupiga ng'ombe ili wafanye kazi na ishara ya nguvu ya mtu kutawala watu wengine.

kiboko cha mkandamizaji wake

Isaya anazungumzia nguvu ya mkandamizaji ambayo anayo juu ya watu wa Yuda kana kwamba kilikuwa kipande cha mbao kilichotumiwa kupiga ng'ombe ili aweze kufanya kazi.

kama katika siku ya Midiani

Neno "siku" ni lahaja ambayo inaweza kumanisha tukio ambalo linachukua zaidi ya siiku moja kufanyika. "kama pale mlipowashinda Wamidiani"

kila buti inayokanyaga katika ghasia na mavazi yaliyobiringishwa katika damu yatachomwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "utachoma buti za wanajeshi na nguo zao, ambazo zimefunikwa na damu"

yatachomwa, mafuta kwa ajili ya moto

Hii inaweza kuwekwa wazi kwa kutafsiri kama sentensi mpya. "kuchomwa. Utafanya buti na mavazi mafuta kwa ajili ya moto"

Isaiah 9:6

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kufafanua kipindi ambapo Mungu atawaokoa watu wa Israeli (9:1). Ingawa matukiio haya yatatokea katika siku za usoni za Isaya, anaelezea kana kwamba yamekwisha tokea. Hii inasisitiza ya kwamba hakika vitatokea.

Kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, kwetu mwana ametolewa

Misemo hii miwili ina maana moja. Neno "yetu" ina maana ya wote msemaji na mskilizaj na kwa hiyo ziko pamoja. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Kwa maana Bwana atatoa kwetu mtoto"

utawala utakuwa juu ya bega lake

"atakuwa na mamlaka ya kutawala kama mfalme" au "Yahwe atamfanya awe na wajibu wa kutawala"

Mshauri

yule ambaye anashauri wafalme

Katika ongezeko la ufalme wake na wa amani hatukauwa na mwisho

"Kadri muda unavyopita atatawala juu ya watu zaidi na zaidi na kuwawezesha kuishi kwa amani zaidi na zaidi"

anapotawala katika kiti cha enzi cha Daudi

Kukaa katika "kiti cha enzi cha Daudi" ni mfano wa maneno ya kuwa na haki ya kutawala; uzao wa Daudi pekee unweza kuwa mfalme juu ya Israeli. "ana haki ya kutawala kama uzao wa Daudi"

ufalme wake, kuuimarisha na kuuhimili kwa haki na kwa haki

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. "ufalme wake". Ataimarisha na kulinda ufalme wake, na atafanya kilicho haki"

Yahwe wa majeshi

Yahwe wa majeshi wa Israeli

Isaiah 9:8

Bwana alituma neno dhidi ya Yakobo, nalo likaanguka juu ya Israeli

"Tuma neno" ina maana ya kuzungumza. "Bwana amezungumza dhidi ya watu wa Israeli"

Yakobo ... Israeli ... Efraimu ... Samaria

Majina haya yana maana ya watu wa ufalme wa kaskazini wa Israeli.

Watu wote watajua, hata Efraimu na wakazi wa Samaria

Kile watakachojua kinaweza kuwekwa wazi. "Watu wote watajua ya kwamba Bwana amewahukumu wao, hata wale wa Efraimu na Samaria"

Matofali yameanguka, lakini tutaijenga tena kwa mawe ya kuchonga; mkuyu umekatwa chini, lakin tutaweka mkangazi katika nafasi yao

Maana kamili inaweza kuwekwa wazi. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Tutarudishia mahali pake matofali ya kawaida ya miji yetu iliyoangamizwa kwa mawe ya gharama ya kuchongwa, na tutapanda miti mikubwa ya mikangazi ambapo miti ya kawaida ya mkuyu iliota"

Isaiah 9:11

Kwa hiyo Yahwe atamuinua dhidi yake Resini, mshindani wake

Hapa "Resini" inawakilisha jeshi lake. "Kwa hiyo, Yahwe atamleta Resini na jeshi lake dhidi ya watu wa Israeli"

Resini

Hili ni jina la mwanamume.

na atawatikisa maadui zake

Msemo "tikisa" ni lahaja ambayo ina maana ya kuwachochea kushambulia. "na Yahwe atasababisha adui wa Israeli kushambulia"

Watameza Israeli kwa mdomo wazi

"Kumeza" ni jinsi ambavyo wanyama pori hula mawindo. "Kama mnyama mwitu anavyokula mawindo yake, jeshi la adui litaangamiza watu wa Israeli"

Katika vitu hivi vyote, hasira yake haipungui; badala yake, mkono wake

"Hata kama vitu hivi vyote vimetokea, bado ana hasira, na mkono wake"

mkono wake bado unanyoshwa nje

Isaya anazungumza kana kwamba Yahwe alikuwa mtu ambaye anataka kumpiga mtu mwingine kwa ngumi yake. Hii ni sitiari kwa ajili ya Yahwe kuadhibu Israeli. "atakuwa tayari kuwaadhibu"

Isaiah 9:13

Yahwe wa majeshi

Yahwe wa majeshi ya Israeli.

kichwa mpaka mkia

Isaya anafafanua sitiari hii katika mstari wa 15. "Kichwa", sehemu ya mnyama ambayo mtu angetaka kuwa, ni "kiongozi na mtu mwadilifu", na "mkia" sehemu chafu ya mnyama, ni "nabii anayefundisha uongo"

tawi la mnazi na matete

"Tawi la mnazi" huota juu ya mti na sitiari kwa ajili ya watu ambao ni muhimu na hutawala wengine. "Tete" huota katika maji ya kina kifupi na sitiari kwa ajili ya watu ambao ni maskini na hawana umuhimu na hutawaliwa na wengine.

Isaiah 9:16

Wale ambao wanaongoza watu hawa wanawapotosha

Viongozii kusababisha watu kutotii inazungumziwa kana kwamba viongozi waliwaongoza katika njia isiyo sahihi. "Viongozi wa Israeli wamesababisha watu kutomtii Mungu"

na wale ambao wanaongozwa wanamezwa

Hii ni sitiari ambayo inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. Maana zaweza kuwa 1) "na wale ambao wanaongozwa wanachanganyikiwa" au 2) "na Yahwe huangamiza wale ambao wanaongoza"

kila kinywa kinazungumza vitu vya kipumbavu

Neno "kinywa" lina maana ya mtu. "kila mtu huzungumza vitu vya kipumbavu"

Katika vitu hivi vyote, hasira yake haipungui; badala yake, mkono wake

"Ingawa vitu hivi vyote vimetokea, bado ana hasira, na mkono wake"

mkono wake bado unanyoshwa nje

Isaya anazungumza kana kwamba Yahwe alikuwa mtu ambaye anataka kumpiga mtu mwingine kwa ngumi yake. Hii ni sitiari kwa ajili ya Yahwe kuwaadhibu Israeli. "bado atakuwa tayari kuwaadhibu"

Isaiah 9:18

Uovu unawaka kama moto; unameza mibigili na miiba; pia unawasha vichaka vya msitu

Matendo ya uovu ya watu yanazungumziwa kana kwamba yalikuwa moto mharibifu kabisa. Moto huu huchoma hata mibigili na miiba, mimea ambayo huota katika maeneo ambayo hawaishi tena, na "vichaka vya msituni" ambapo hakuna mtu aliyewahi kuishi, kwa sababu ulikuwa umeangamiza maeneo ambapo watu walikuwa wakiishi.

mibigili ... miiba

Maneno "mibigili" na "miiba" yote ina maana mimea ya miiba isiyo na thamani; inaweza kutafsiriwa kutumia neno moja. "vichaka vya miiba"

Katika ghadhabu ya Yahwe wa majeshi nchi inachomwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Kama moto ambao unachoma nchi, hasira kali ya Bwana itaangamiza watu wa Israeli"

Hakuna mtu amwachaye ndugu yake

"Hakuna mtu afanyaye kitu chochote kusaidia mtu mwingine yeyote kutoroka"

Isaiah 9:20

Watanyakua chakula katika mkono wa kuume ... katika mkono wa kushoto

Msemo huu una maana ya kwamba watu watanyakua chakula popote watakapokikuta.

Kila mmoja hata atakula nyama ya mkono wake mwenyewe

Maana zaweza kuwa 1) watu watakuwa na njaa sana hadi watataka kula au hatimaye watakula mikono yao wenyewe au 2) neno "mkono" ni sitiari kwa ajili ya jirani wa mtu.

Katika vitu hivi vyote, hasira yake haipungui; badala yake, mkono wake

"Ingawa vitu hivi vyote vimetokea, bado ana hasira, na mkono wake"

mkono wake bado unanyoshwa nje

Isaya anazungumza kana kwamba Yahwe alikuwa mtu ambaye anataka kumpiga mtu mwingine kwa ngumi yake. Hii ni sitiari kwa ajili ya Yahwe kuwaadhibu Israeli. "bado atakuwa tayari kuwaadhibu"

Isaiah 10

Isaiah 10:1

kwa wale ambao hufanya sheria zisizo za haki na kuandika maagizo yasiyo ya haki

Misemo hii miwili ina maana moja. "kwa wale ambao hutengeneza sheria na maagizo ambayo sio haki kwa wote"

Watawanyima wahitaji haki, kunyanganya maskini wa watu wangu haki zao

Misemo hii miwili ina maana moja. "hazina haki kwa maskini na wahitaji miongoni mwa watu wangu"

wahitaji

"watu maskini"

kupora wajane

"chukua kila kitu kutoka kwa wanawake ambao waume zao wameshakufa"

na kufanya wasio na baba mawindo yao

Isaya inalinganisha yatima kwa wanyama ambao wanyama wengine huwinda na kula. Hii inasisitiza ya kwamba yatima hawana uwezo na waamuzi wanaweza kuwadhuru kiurahisi. "na kuwadhuru watoto ambao hawana wazazi kama mnyama anayemfuata windo lake"

mawindo

wanyama ambao wanyama wengine hutaka kuwshika na kuwala

Isaiah 10:3

Mtafanya nini katika siku ya hukumu ... mbali?

Isaya anatumia swali kukaripia wale ambao Yuda anadhuru maskini na watu dhaifu. "Utaweza kutofanya kitu katika siku ya hukumu ... mbali!"

siku ya hukumu

"siku ambayo Yahwe anakuja kukuhukumu" au "siku ambayo Yahwe anakuadhibu"

Utatoroka kwa nani kwa ajili ya msaada, na utaacha utajiri wako wapi?

Isaya anatumia swali kukaripia wale ambao wapo yuda ambao hudhuru maskini na watu dhaifu. "Hauna sehemu ya kukimbilia kwa msaada, na hautakuwa na sehemu ya kuficha utajiri wako!"

Hakuna kinachobaki

"Hakuna kitu kinachobaki kwa ajili yako kufanya"

na unajikunyata miongoni mwa wafungwa au kuanguka miongoni mwa waliouliwa

"'na adui zako watakuchukua kama wafungwa au watakuua"

Katika haya yote, hasira yake haishuki

"Hata kama vitu hivi vyote vikitokea, bado ana hasira".

mkono wake bao unanyoshwa nje

Isaya anazungumza kana kwamba Yahwe alikuwa mtu aliyetaka kumpiga mtu mwingine kwa ngumi yake. Hii ni sitiari kwa ajili ya Yahwe kuadhibu Israeli. "atakuwa tayari kuwaadhibu"

Isaiah 10:5

Ole

neno hili linaweka alama mwanzo wa tangazo la Mungu kuhusu adhabu kali dhidi ya Ashuru.

Ashuru

Hii ina maana ya mflame wa Ashuru.

rungu ya hasira, fimbo ambayo ninatawala ghadhabu yangu

Misemo hii miwili ina maana moja. Yahwe analinganisha mfalme wa Ashuru kwa silaha ambayo mtu hubeba mkononi na kupiga watu wengine. Inasisitiza ya kwamba mfalme wa Ashuru na jeshi lake ni chombo ambacho Yahwe hutumia kuadhibu Israeli. "nani atakuwa kama silaha mikononi mwangu ambayo nitaitumia kuponyesha hasira yangu"

ninamtuma ... ninamuamuru

Neno "ninamtuma" hapa pia ina maana ya mflame wa Ashuru. Lakini haimaanishi Mungu anamtuma mfalme pekee; anamtuma pamoja na jeshi la Ashuru. "Ninatuma jeshi la Ashuru ... ninawaamuru"

dhidi ya taifa lenye kiburi na dhidi ya watu ambao wanabeba ghadhabu yangu ya kumwagikia

"kushambulia taifa lililojaa watu wenye kiburi ambao wamenifanya niwe na hasira sana"

ambao wanabeba ghadhabu yangu ya kumwagikia

Yahwe anazungumzia ghadhabu yake kana kwamba ilikuwa kimiminiko kuzidi chombo ambacho kilibeba; "watu" wanajaribu kubeba chombo chake, lakini ni kizito, na Yahwe anamwaga kimiminiko ndani hata baada ya kuanza kumwagikia nje. "ambao ninaendela kuwa na hasira nao hata baada ya kuwaadhibu"

kuchukua mateka

"kuchukua kila kitu walichonacho"

kuchukua mawindo

kuwachukua watu kama mawindo.

kuwakanyaga kama tope

Maana zaweza kuwa 1) Yahwe analinganisha jeshi la Ashuru kushambulia Israeli na watu kukanyaga katika tope ambao hawajali nini kinatokea kwa matope. "wakanyage mpaka wawe kama matope" au 2) watu wanakanyaga juu ya watu wengine kwa hiyo wanalala kwenye matope na kushindwa kuinuka. Hii ni sitiari ya kuwashinda kabisa. "kuwashinda kabisa"

Isaiah 10:7

Lakini hivi sivyo kile anachokusudia, wala hawazi kwa namna hii

Maana ya "hivi" na "namna hii" zinaweza kuwekwa wazi. "lakini mfalme wa Ashuru hakusudii kufanya kile ninachomuambia, na wala hafikirii ya kwamba ninamtumia kama silaha"

Ni katika moyo wake kuangamiza na kuondoa mataifa mengi

Maneno "angamiza" na "ondoa" ina maana moja. Zinatumiwa kwa ajili ya msisitizo. "Anataka uangamize kabisa mataifa mengi"

Je! wakuu wangu wote sio wafalme?

Mfalme wa Ashuru anatumia swali kusisitiza kile anachoamini kila mtu anatakiwa kuwa anakifahamu. "Nimefanya makapteni kutoka kwa wafalme wa jeshi langu juu ya nchi nilizozishinda!"

Je! Kalno sio kama Karkemishi? Hamathi sio kama Arpadi? Je! Samaria sio kama Damesk?

Mfalme wa Ashuru anatumia maswali haya kwa ajili ya msisitizo. "kalno sio tofauti na Karkemishi. Hamathi sio tofauti na Arpadi. Samaria sio tofauti na Dameski. Nimezishinda zote!"

Kalno ... Karkemishi ...

Haya ni majina ya miji.

Isaiah 10:10

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kunukuu kile mfalme wa Ashuru anachosema.

Kama mkono ulivyoshinda

"Mkono" ni kumbukumbu kwa nguvu ya jeshi. "Kama jeshi langu lenye nguvu lilivyoshinda" au "Kama nilivyoshinda"

wangu

Hii ina maana ya mfalme wa Ashuru.

ambao sanamu zao za kuchonga zilikuwa kubwa kuliko

Katika kipindi hiki watu waliamini ya kwamba ukubwa wa sanamu ulionyesha jinsi ufalme ulivyokuwa na nguvu ambayo iliijenga. Mfalme wa Ashuru kusema kuwa kwa sababu sanamu katika Yerusalemu sio kubwa kama sanamu za falme alizozishinda, Yerusalemu ingekuwa na uwezo mdogo zaidi kumshinda kuliko zingine.

kama nilivyofanya kwa Samaria na sanamu zake sizizo na thamani

Neno "Samaria" lina maana ya watu ambao waliishi pale, na "zake" ina maana ya mji wa Samaria. Miji na mataifa mara kwa mara ilizungumziwa kana kwamba ilikuwa wanawake. "'kama nilivyofanya kwa watu wa Samaria na sanamu zao sizizo na thamani"

sitafanya hivyo hivyo pia kwa Yerusalemu na kwa sanamu wake?

Mfalme wa Ashuru anatumia swali kusisitiza uhakika ya kwamba atashinda watu wa Israeli. "Hakika nitafanya kile kile kwa Yerusalemu na sanamu wake!"

Isaiah 10:12

Bwana atakapomaliza kazi yake juu ya Mlima Sayuni na juu ya Yerusalemu, nitaadhibu

Yahwe anajizungumzia kana kwamba alikuwa mtu mwingine. "Pale Mimi, Bwana, nitakapomaliza kazi yangu juu ya Mlima Sayuni na juu ya Yerusalemu, nitaadhibu"

kazi yake juu ... na juu ya

kazi yake ya kuadhibu. "kuadhibu ... na kuadhibu"

Nitaadhibu usemi wa moyo wa kujisifu wa mfalme wa Ashuru na muonekano wake wa kiburi

"Nitaadhibu mfalme wa Ashuru kwa ajili ya mambo ya kiburi aliyosema na muonekano wa kiburi katika uso wake"

Kwa maana anasema

"Kwa maana mfalme wa Ashuru anasema"

Nimeondoa mipaka ya watu

Hapa neno "nimeondoa" ina maana ya mfalme wa Ashuru. Alikuwa kiongozi wa jeshi la Ashuru na kuchukua sifa kwa kile jeshi lilifanya kwa amri yake. "jeshi langu limeondoa mipaka ya watu"

kama ng'ombe dume

"na nguvu kama ng'ombe dume". Baadhi ya tafsiri husoma, "kama mwanamume mwenye nguvu"

Nimewaweka chini

"Mimi na jeshi langu tumewaweka"

Nimewaweka chini wakazi

Maana zaweza kuwa 1) mfalme wa Ashuru amewaaibisha watu wa nchi alizozishinda au 2) ameondoa wafalme wa mataifa ili zisiweze kutawala tena.

Isaiah 10:14

Maelezo ya Jumla

Yahwe bado anamnukuu mfalme wa Ashuru.

Mkono wangu umekamata

Mkono ni mfano wa maneno kwa nguvu ya mfalme au jeshi lake. "Katika nguvu yangu nimekamata" au "Mkono wangu umekamata"

Mkono wangu umekamata, kama katika kiota, utajiri wa mataifa

Mfalme wa Ashuru analinganisha kuchukua hazina kutoka katika mataifa kwa mtu anayechukua mayai nje ya kiota cha ndege. Hii inasisitiza jinsi ilivyo rahisi kwake na jeshi lake kushinda falme hizi zingine. "Jeshi langu limeiba utajiri kutoka mataifa kwa urahisi kama mwanamume anayechukua mayai kutoka kwenye kiota"

na kama mtu anayekusanya mayai yaliyotelekezwa, nilikusanya dunia yote

"na vile tu kama mtu anayechukua mayai kutoka katika kiota pale ndege hayupo kuyalinda, jeshi langu limechukua hazina ya kila taifa"

Hakuna aliyepigapiga mabawa au kufungua mdomo wao au kulia

Hii inalinganisha mataifa kwa ndege ambaye hukaa kwa utulivu huku mayai yake yanachukuliwa. Hii inasisitiza ya kwamba mataifa hayakufanya kitu wakati jeshi la Ashuru lilipochukua mali zao zote. "Na kama ndege ambaye hatoi sauti au kupiga mabawa yake pale mtu anapoiba mayai yake, mataifa hayakufanya chochote tulipokuwa tukichukua hazina zao"

Isaiah 10:15

Je! shoka litajivunia lenyewe dhidi ya yule anayelitumia? Je! msumeno utajisifu zaidi kuliko yule anayekata kwa kulitumia?

Msemaji anatumia maswali haya kukejeli mfalme wa Ashuru. "Shoka haliwezi kujivuna ya kwamba ni bora kuliko yule anayelishikilia. Na msumeno haupati utukufu zaidi ya yule anayekata kwa kulitumia"

msumeno

kifaa chenye ncha kali kiinchotumiwa kukata mbao

Ni kana kwamba kiboko kinaweza kuwainua wale ambao huiinua, au kana kwamba rungu ya mbao inaweza kumuinua mtu

Misemo hii ina maana moja na inatumika kuimarisha maana ya maswali mawili kabla yao. Inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. "Na wala fimbo au gongo haviwezi kumwinua yule anayeziokota"

Kwa hiyo Bwana Yahwe wa majeshi atatuma udhoofishaji katika mahodari wake wa juu

Haipo wazi kama Yahwe au Isaya anazungumza. Hii inaweza kuandikwa ili kwamba nomino dhahania "kudhoofika" inaelezwa kama kitenzi "kufanya dhaifu". Kwa hiyo, Mimi, Bwana wa Yahwe wa majeshi, atafanya wanajeshi wenye nguvu wa mfalme kuwa dhaifu"

chini ya utukufu wake kutachochewa mwako kama wa moto

Yahwe analinganisha adhabu yake kwa moto. Hii inasisitiza ya kwamba adhabu yake utaangamiza kabisa ufahari wote na ukubwa wa ufalme wa Ashuru. "Nitaangamiza ukubwa wake kana kwamba nilikuwa nikianzisha moto kuchoma kila kitu anachojivunia"

Isaiah 10:17

Nuru ya Israeli itakuwa moto

Msemo "nuru ya Israeli" ina maana ya Yahwe. Haipo wazi kama Yahwe an Isaya anazungumza. "Mimi, Yahwe, nuru ya Israeli, atakuwa kama moto"

moto

"Moto" unasisitiza nguvu ya Yahwe kuangamiza kila kitu ambacho hakimpi utukufu.

Mtakatifu wake mwale

"Mimi, Yahwe, Mtakatifu wa Israeli, atakuwa kama mwale".

utaunguza na kumeza miiba na mibigili yake

"Moto utaunguza na kumeza miiba na mibigili ya mfalme wa Ashuru" Msemaji analinganisha jeshi la mfalme wa Ashuru kwa miiba na mibigili. Hii inasisitiza ilivyo rahisi kwa Mungu kuwaangamiza. "Nitaangamiza Ashuru kama moto unaochoma miiba na mibigili"

miiba ... mibigili

Maneno "mibigili" na "miiba" yote yana maana mimea isiyo na thamani y miiba; inaweza kutafsiriwa kutumia msemo mmoja.

Yahwe atateketeza utukufu wa msitu wake na nchi yake inayozaa

Maana zaweza kuwa 1) "Yahwe ataangamiza misitu mikubwa na mshamba katika taifa la Ashuru" au 2) "Yahwe ataangamiza jeshi la Ashuru kama moto unavyochoma misitu mikubwa na mashamba"

zote nafsi na mwili

Maana zaweza kuwa 1) hii inasisitiza ya kwamba Mungu ataangamiza kabisa misitu na mshamba. "kabisa" au 2) hii ina maana Mungu atangamiza kabisa watu wa Ashuru. Msemo "nafsi na mwili" ina maana ya sehemu ya roho na sehemu ya mwili ya mtu.

itakuwa kama pale maisha ya mtu mgonjwa unavyotokomea

Hii inalinganisha aidha misitu na mashamba ya Ashuru au jeshi la Ashuru kwa mtu mgonjwa anapolala kitandani akifa. Hii inasisitiza jinsi jambo kubwa sana linaweza kuwa dhaifu na kufa. "watakuwa kama mtu mgonjwa anayekuwa dhaifu na kufa"

Masalio ya miti y msitu wake utakuwa mchache sana

"Vile vinavyosalia vya miti katika msitu wa mfalme vitakuwa vichache sana"

Isaiah 10:20

Katika siku hiyo

Hii ina maana kipindi ambacho Mungu anafanya mambo ambayo yanaelezwa katika 10:15. "Katika kipindi hicho"

ambayo imetoroka

Maana inaweza kuwekwa wazi. "ambaye ametoroka kutoka katika jeshi la Ashuru"

haitategemea tena kwa yule ambaye aliwashinda

"hatategemea tena mfalme wa Ashuru, ambaye aliwadhuru"

Mtakatifu

Mtakatifu wa Israeli

Isaiah 10:22

watu wako, Israeli, ni

Hapa "wako" ni umoja. Tafsiri zinazowezekana ni 1) Mungu anazungumza kwa Isaya na "wako" ina maana ya Isaya. "watu wako Israeli ni" au 2) Isaya au Mungu anazungumza kwa taifa la Israeli na "wako" ina maana ya taifa. "watu wako, O Israeli, ni"

ni kama mchanga wa pwani

Hii inasisitiza ya kwamba kulikuwa na idadi kubwa ya watu wa Israeli. "ni wengi mno kuhesabu, kama mchanga wa pwani"

Uharibifu umeagizwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe ameagiza ya kwamba ataangamiza wengi wa wale wanaoshi Israeli"

kadri haki inayomwagikia inavyodai

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. "Hii inapaswa kufanywa kwa ajili ya haki timilifu" au "Yahwe anatakiwa kufanya hili kwa sababu ni mwenye haki kabisa"

kutekeleza uharibifu uliobainishwa katika nchi

Maana zaweza kuwa 1) "kuangamiza kila kitu katika nchi kama alivyoamua kufanya" au 2) "kuangamiza watu katika nchi kama alivyoamua kufanya"

uliobainishwa

"kuamuliwa"

Isaiah 10:24

Ashuru

Isaya anazungumzia mfalme wa Ashuru na jeshi lake kana kwamba alikuwa mtu mmoja. "mfalme wa Ashuru na jeshi lake"

Atakupiga kwa fimbo na kuinua gongo lake dhidi yako

Neno "lake" ina maana ya "Ashuru", utambulisho wa mfalme wa Ashuru na jeshi lake. Maneno "fimbo" na "gongo" ina maana ya vipande vya mbao ambavyo watu hutumia kama rungu kupiga wanyama na watu wengine. Isaya anazungumzia njia ambayo Ashuru atatawala juu ya Waisraeli kana kwamba Ashuru alikuwa akiwapiga Waisraeli kwa rungu. "Ashuru atatawala juu yako na kukufanya mtumwa"

kama Mmisri alivyofanya

Maana kamili inaweza kuwekwa wazi. "kama Wamisri walivyotawala juu ya mababu zako na kuwafanya watumwa"

hasira yangu utapelekea uharibifu wake

Nomino dhahania "uharibifu" unaweza kutafsiri kama kitenzi. "Nitamwangamiza kwa sababu nina hasira juu yake"

Isaiah 10:26

Yahwe wa majeshi

Yahwe wa majeshi wa Israeli

atainua mjeledi dhidi yao

"atapiga Ashuru kwa mjeledi". Mungu hatatumia mjeledi kihalisia. Hii ina maana ya nguvu ya Mungu kuadhibu Ashuru kwa ukalii. "nitaadhibu Ashuru kwa ukali kana kwamba kwa mjeledi"

kama pale alipowashinda Midiani katika mwamba wa Orebu

Hii ina maana ya pale Mungu alipomsaidia mtu aliyeitwa Gideoni kuwashinda jeshi la Midani.

Atainua fimbo yake juu ya bahari na kuinua kama alivyofanya kwa Misri

Hii ina maana ya fimbo pale Mungu aliposababisha maji ya Bahari ya Shamu kugawanyika ili watu wa Israeli waweze kutoroka kutoka kwa jeshi la Misri na ili kwamba jeshi la Misri lizame ndani yake. "Atakusaidia kutoroka kutok katika jeshi la Ashuru kama alivyowasaidia mababu zako kutoroka jeshi la Misri"

mzigo wake unainuliwa kutoka kwenye bega lako na nira yake kutoka shingoni mwako

"Yahwe atabeba mzigo ambao Ashuru ameweka katika bega lako, na atatoa nira ambayo wameweka juu ya shingo yako". Misemo hii miwili ina maana moja. Maneno "mzigo" na "nira" ina maana ya utumwa. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe ataondoa Ashuru ambaye huwakandamiza na atawazuia kuwafanya kuwa watumwa"

nira itaangamizwa kwa sababu ya unene

Msemo huu unaashiria ya kwamba shingo ya mnyama ambayo inavaa nira itakuwa nene sana kutosha nira tena. Hii ni sitiari kwa Israeli kuwa na nguvu sana hadi Ashuru kutowatawala tena. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "shingo yako itakuwa nene sana hadi itavunja nira" au "mtakuwa na nguvu sana hadi hamtakuwa tena watumwa wa Ashuru"

Isaiah 10:28

amekuja ... amepita ... ametunza ... wamevuka ... kupanga ... hutetemeka ... amekimbia

Isaya anazungumzia matukio haya ya mbeleni kana kwamba yamekwisha tokea.

Aiath ... Migroni ...Mikmashi ... Geba ... Rama ... Gibea

Hii yote ni miji na vijiji karibu na Yerusalemu ambazo jeshi la Ashuru lilipita katikati na kusababisha shida.

Rama hutetemeka na Gibea wa Sauli amekimbia

"Watu wa Rama hutetemeka na watu wa Gibea wa Sauli wamekimbia"

Isaiah 10:30

binti wa Galimu

Neno "binti" hapa lina maana ya watu ambao huishi katika mji. "Galimu" au "watu wa Galimu"

Galimu ... Laisha ... Anathothi ... Madmena ... Gedimu ... Nobu

Haya ni majina ya miji zaidi na vijiji karibu na Yerusalemu ambayo jeshi la Ashuru lilisafiri katikati kusababisha hofu miongoni mwa watu. Zote hizi zina maana ya watu ambo huishi katika maeneo haya.

atasimama Nobu na kutikisa ngumi yake

Hapa "atasimama" na "yake" ina maana ya mfalme wa Ashuru na wanajeshi wake. Watu walikuwa wakitikisa ngumi zao kwa watu ambao walikuwa wakiwatisha. "jeshi la Ashuru litasimama Nobu na kutisha"

mlima wa binti wa Sayuni, kilima cha Yerusalemu

Maneno "mlima" na "kilima" ni mfano wa maneno kwa ajili ya watu ambao wanaishi ndani yao. "watu wa Mlima Sayuni na watu wanaoishi katika kilima kilicho Yerusalemu". Maneno "mlima wa binti wa Sayuni" ina maana ya kitu kimoja kama maneno "kilima cha Yerusalemu".

Isaiah 10:33

Tazama

HIi inaweza kutafsiriwa kama "Angalia" au "'Sikiliza" au "Zingatia kwa makini kile ninachotaka kukuambia".

Yahwe wa majeshi

Yahwe wa majeshi ya Israeli

atapogoa matawi ... na Lebanoni katika ufahari wake utaanguka

Isaya anazungumzia jeshi la Ashuru kana kwamba lilikuwa miti mirefu katika Lebanoni. Mungu ataangamiza jeshi kama watu wanvyokata chini miti mikubwa ya Lebanoni. Hii inasisitiza ya kwamba ingawa jeshi lina nguvu, Mungu ana uwezo wa kuliangamiza.

atapogoa matawi

"atakata matawi makubwa ya miti". Ataangamiza jeshi la Ashuru kama wanamume wenye nguvu wanavyokata matawi makubwa ya miti"

kwa kishindo cha kutisha

Hii inaweza kuandikwa ili kwamba nomino dhahania "kishindo" inaelezwa kama kitenzi "kupiga kelele". "na matawi yataanguka chini katika ardhi na kutoa sauti ya kutisha" au "na matawi yataanguka katika ardhii kwa sauti kubwa sana"

miti mirefu zaidi itakatwa chini

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "'atakata chini miti mirefu zaidi"

miti mirefu zaidi

Hii ni sitiari kwa ajili ya "wanajeshi wenye nguvu zaidi"

wenye kiburi watashushwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "atawashusha chini watu wenye kiburi"

wenye kiburi

mjivuno

vichaka vya msitu

"vichaka vinene katika msitu". Hii inawezekana kuwa sitiari kwa wale watu ambao hawajulikani"

Lebanoni katika ufahari wake utaanguka

"misitu ya Lebanoni haitakuwa mikubwa tena". Hii inaweza kuwa sitiari kwa ajili ya jeshi la Ashuru. "Yahwe atawashinda jeshi la Ashuru, kama jinsi lilivyo na nguvu"

Isaiah 11

Isaiah 11:1

Chipukizi litachipuka kutoka kwenye kisiki cha Yese ... tawi kutoka katika mizizi yake litazaa matunda

Isaya anamzungumzia Yese na uzao wake kana kwamba walikuwa mti ambao ulikuwa umekatwa chini. Misemo hii miwili inaelezea juu ya uzao wa Yese ambaye atakuwa mfalme. "Kama vile chipukizi linavyochipuka kutoka kwenye kisiki cha mti, vile vile uzao wa Yese utakuja kuwa mfalme juu ya kinachobaki cha Israeli"

kisiki cha Yese

Kisiki ni kile kinachobaki kwenye mti baada ya kukatwa chini. "Kisiki" cha Yese kinawakilisha kile kinachobaki katika ufalme ambao mwana wa Yese Daudi aliwahi kuwa mfalme.

Roho wa Yahwe atatua juu yake

Kutua juu yake inawakilisha kuwa pamoja naye na kumsaidia. Neno "yake" ina maana ya yule ambaye angekuja kuwa mfalme.

roho ya hekima ... roho ya mafunzo ... roho ya maarifa ... hofu ya Yahwe

Hapa neno "roho" ina maana ya uwezo au sifa ambayo Roho wa Yahwe angempatia. "na atasababisha kuwa na hekima na uelewa, mafunzo na uwezo, maarifa na hofu ya Yahwe"

Isaiah 11:3

Kauli Unganishi

Isaya anaendelea kumfafanua mfalme.

hatahukumu kwa kile ambacho macho yake yanaona

Msemo "kile ambacho macho yake yanaona" ina maana ya kuona vitu ambavyo sio muhimu kwa kuhukumu mtu kwa sahihi. "hatahukumu mtu kwa kumtazama tu vile ambavyo mtu anavyoonekana"

wala kuamua kwa kile masikio yake yanasikia

"na hataamua kwa kile ambacho masikio yake husikia". Msemo "kile ambacho masikio yake husikia" yana maana ya kusikia kile ambacho watu wanasema juu ya mtu. "na hatahukumu mtu kwa kusikia kile ambacho wengine wanasema juu yake"

maskini ... wanyenyekevu ... waovu

Misemo hii ina maana ya watu ambao wana sifa hizi. "watu maskini ... watu wanyenyekevu ... watu waovu"

Ataipiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake ... kwa pumzi ya midomo yake atawachinja waovu

Misemo hii miwili kimsingi ina maana moja.

Ataipiga nchi kwa fimbo ya kinywa chake

Neno "nchi" hapa linawakilisha watu wa dunia. Kuwapiga kwa fimbo ya kinywa chake inawakilisha kuwahukumu, na hukumu hiyo italeta adhabu. "Atahukumu watu wa dunia, na wataadhibiwa"

kwa pumzi ya midomo yake atawachinja waovu

"pumzi ya midomo yake" inawakilisha yeye kuwahukumu. "atahukumu watu waovu, nao watauwawa"

mkanda wa kiuno chake ... mkanda unaozunguka kiunoni kwake

Maana zaweza kuwa 1) mkanda unatumika kuimarisha nguo za mtu ili aweze kufanya kazi, au 2) mkanda ni nguo ya ndani, au 3) mkanda ni mshipii ambao mfalme huvaa kuonyesha mamlaka yake.

Haki itakuwa mkanda wa kiuno chake

Kuvaa haki kama mkanda inawakilisha kuwa mwenye haki. Maana zaweza kuwa 1) haki ya mfalme itamuwezesha kutawala. "Haki yake itakuwa kama mkanda unaozunguka kiuno chake" au 2) haki ya mfalme itaonyesha mamlaka yake ya kutawala. "Atatawala kwa haki"

uaminifu mkanda unaozunguka nyonga yake

Maneno "utakuwa" inaeleweka katika msemo huu. "uaminifu utakuwa mkanda unaozunguka nyonga yake"

uaminifu mkanda unaozunguka nyonga yake

Kuvaa uaminifu kama mkanda inawakilisha kuwa mwaminifu. Maana zaweza kuwa 1) uaminifu wa mfalme utamwezesha kutawala, au 2) uaminifu wa mfalme utaonyesha mamlaka yake ya kutawala. "uaminifu wake utakuwa kama mkanda unaozunguka nyonga yake" au "atatawala kwa uaminifu"

Isaiah 11:6

Taarifa ya Jumla

Isaya anafafanua kile ambacho dunia itakavyokuwa mfalme atakavyotawala. Kutakuwa na amani kamili duniani. Hii inaonyeshwa kwa amani ambayo itakuwepo hata kwa wanyama. Wanyama ambao kawaida huwaua wanyama wengine hawatawaua, na watakuwa salama pamoja.

Mbwa mwitu ... chui ... simba mchanga ... dubu ... Simba

Misemo hii ina maana ya hawa wanyama kwa ujumla, sio kwa mbwa mwitu au chui bayana. Hawa ni wanyama wenye nguvu ambao hushambulia na kula wanyama wengine. "Mbwa mwitu ... chui .. simba wachanga ... dubu ... Simba"

mwanakondoo ... mbuzi mchanga ... ndama ... ndama aliyenenepeshwa ... Ng'ombe ... maksai

Misemo ina maana ya wanyama hawa kwa ujumla, sio mwanakondoo au mbuzi bayana. Hawa wote ni wanyama ambao hula nyasi na majani makavu. Wanyama wengine mara nyingine huwashambulia na kuwala. "mwanakondoo ... mbuzi mchanga ... ndama ... ndama aliyenenepeshwa ... Ng'ombe ... maksai"

chui

paka mkubwa mwenye manyoya ya njano na madoa meusi ambaye huwaua na kuwala wanyama wengine.

ndama, simba mchanga na ndama aliyenenepeshwa, kwa pamoja

Msemo "watakuwa" unaeleweka. ndama, simba, na ndama aliyenenepeshwa watakuwa pamoja

dubu

mnyama mkubwa sana mwenye nywele nene na makucha makali ambaye huwaua na kuwala wanyama wengine.

mtoto mdogo atawaongoza

Mtoto atawatunza na kuwaongoza katika sehemu nzuri kunywa maji na kula nyasi au nyasi kavu.

watachunga pamoja

"watakula nyasi pamoja"

watoto wao

Hii ina maana ya watoto wa wanyama muda mfupi baada ya kuzaliwa.

Isaiah 11:8

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kufafanua amani kamili katika dunia pale mfalme atakapotawala.

mtoto mchanga atacheza juu ya shimo la nyoka

Inaweza kuwekwa wazi ya kwamba mtoto mchanga atakuwa salama kwa sababu nyoka hatamng'ata. "Watoto wachanga watacheza kwa usalama juu ya shimo la nyoka"

nyoka ... tundu la nyoka

Misemo hii ina maana ya nyoka wenye sumu kwa ujumla. "nyoka ... matundu ya nyoka"

mtoto aliyeachishwa ziwa

mtoto ambaye hanywi tena maziwa ya mama yake

katika milima yangu mitakatifu

"Mlima mtakatifu" ni Mlima Sayuni, katika Yerusalemu. "katika mlima mtakatifu wote wa Yahwe"

dunia itakuwa imejaa maarifa ya Yahwe

Msemo "maarifa ya Yahwe" yanawakilisha watu wanaomjua Yahwe. "dunia itakuwa imejaa wale ambao wanamjua Yahwe" au "wale ambao wanamjua Yahwe watafunika dunia"

kama maji yanavyofunika bahari

Msemo huu unatumika kuonyesha jinsi dunia itakavyojaa na watu ambao wanamjua Yahwe. Inaweza kuwa wazi ya kwamba inafanya hivi kama maneno yanafanana na maneno katika msemo uliopita. "kama bahari zilivyojaa na maji"

Isaiah 11:10

mzizi wa Yese

Hii ina maana ya uzao wa Yese na Mfalme Daudi ambaye atakuja kuwa mfalme ambaye alizungumziwa katika 11:1. "Uzao wa wa Yese mfalme" au "mfalme alitokana kwa Yese"

itasimama kama bango kwa ajili ya watu

bango ni bendera ambayo mfalme huinua kama ishara kwa watu kuiona na kuja kwake. "utakuwa kama ishara kwa ajili ya watu" au "itavuta watu kuja kwake"

mataifa

"watu wa mataifa"

Bwana atanyosha tena mkono wake kurejesha aliyesalia wa watu wake

Mkono ni marejeo ya nguvu ya Mungu. "Bwana atatumia tenanguvu yake kuwaleta waliosalia wa watu wake"

Pathrosi ... Elamu .. Hamathi

Haya ni majina ya mahali

Isaiah 11:12

Ataandaa bango kwa ajili ya mataifa

Maana zaweza kuwa 1) "Bwana ataandaa mfalme kama bango kwa ajili ya mataifa" au 2) "Mfalme ataandaa bango kwa ajili ya mataifa"

bango kwa ajili ya mataifa

"bendera kwa ajili ya mataifa kuona" au "bendera kuwaita mataifa kwa ajili yake"

waliotawanywa wa kutoka Yuda

"watu wa Yuda ambao walitawanyika duniani kote"

kutoka pembe nne za dunia

Dunia inapewa taswira ya kwamba ina pembe nne, na pembe hizo ndizo umbali mkubwa kabisa. Hii ina maana ya kila sehemu duniani ambao watu hao wanaweza kuwepo. "kutoka hata sehemu za mbali kabisa za dunia" au "kutoka duniani kote"

Atageuza upande wivu wa Efraimu

Efraimu hapa ina maana ya uzao wa ufalme wa kaskazini wa Israeli. Nomino "wivu" inaweza kuelezwa kama kivumishi. "Atawazuia watu wa Efraimu kutokuwa na wivu"

Yuda hatakuwa na uadui tena kwa Efraimu

Yuda hapa ina maana ya uzao wa ufalme wa kusini wa Israeli. Msemo huu unaweza kuwekwa katika halii ya kutenda. "atawazuia watu wa Yuda kutokuwa na uadui" au "atawazuia wtu wa Yuda kutochukia"

Isaiah 11:14

watashuka chini kwa kasi juu ya vilima vya Wafilisti

Watu wa Israeli na Yuda wanawekewa taswira kana kwamba wao ni ndege ambao wanaweza kupaa chini kwa haraka kumshambulia mtu au mnyama. "watakwenda kwa haraka katika vilima vya Wafilisti kushambulia watu kule"

ghuba ya Bahari ya Misri

"ghuba" ni eneo kubwa la maji ambalo huzungukwa kidogo na nchi kavu.

Kwa upepo wake unaochoma atapunga mkono wake juu ya Mto Frati

Kupunga mkono juu ya kitu inawakilisha nguvu yake kuibadili. "Kwa nguvu yake atasababisha upepo uchomao kuvuma juu ya Mto Frati"

upepo wake unaochoma

Huu ni upepo wenye nguvu na wa moto ambao husababisha sehemu ya maji katika mto kukauka.

ili iweze kuvukwa juu kwa ndara

"ili kwamba watu waweze kuvuka juu hata kama wanavaa ndara zao"

Isaiah 11:16

Kutakuwa na njia

Njia ni barabara kubwa ambayo watu wengi wanaweza kusafiri juu yake."Yahwe atafanya barabara"

katika ujio wao kutoka katika nchi ya Misri

"walipokuja kutoka katika nchi ya Misri"

Isaiah 12

Isaiah 12:1

Taarifa ya Jumla

Hapa Isaya anaendelea kuelezea jinsi itakavyokuwa pale mfalme ambaye Mungu amemchagua anatawala.

Katika siku hiyo

Inaweza kuwekwa wazi ni wakati gani unaomaanishwa. "Katika kipindi hicho" au "Pale mfalme anapotawala"

hasira yako imegeuka

Hasira ya Mungu inazungumziwa kana kwamba mtu anaweza kugeuka na kuondoka. Ina maana ya kwamba Mungu ameacha kuwa na hasira. "Hauna hasira na mimi tena"

Mungu ni wokovu wangu

Mungu anasababisha wokovu wa mtu inazungumziwa kana kwamba Mungu alikuwa huo wokovu. Nomino dhahania "wokovu" inaweza kuelezwa na nomino "mwokozi" au kitenzi "okoa". "Mungu husababisha wokovu wangu" au "Mungu ni mwokozi wangu" au "Mungu ndiye anayeniokoa"

Yahwe ni nguvu yangu

Mungu kusababisha mtu kuwa na nguvu inazungumziwa kana kwamba Yahwe alikuwa nguvu yao. "Yahwe hunifanya niwe na nguvu"

na wimbo

Neno "wimbo" hapa linawakilisha kile mtu anachokiimba. "na yule ambaye nayemwimba kwa furaha"

Amekuwa wokovu wangu

"Ameniokoa"

Isaiah 12:3

Kwa furaha utateka maji kutoka kwenye visima vya wokovu

Isaya anazungumzia watu kukombolewa kana kwamba walikuwa wakipata wokovu kwa namna ambavyo watu hupata maji kutoka kisimani. "utafurahi pale atakapokukomboa, kama watu wanavyofurahi wanapoteka maji kutoka kisimani"

kuliita jina lake

Hapa "jina lake" lina maana ya Yahwe. Kuliita jina lake lina maana ya aidha kumsifu au kumwomba msaada. "kumsifu kwa sauti" au "kumwita akusaidie"

kutamka matendo yake miongoni mwa watu

Nomino ya "matendo" inaweza kuelezwa na msemo "kile aliuchofanya". "Waambie watu juu ya mambo makubwa aliyofanya"

kutamka ya kuwa jina lake limeinuliwa

Hapa "jina lake" lina maana ya Yahwe. "tangaza ya kuwa ameinuliwa" au "tangaza ya kwamba ni mkuu"

Isaiah 12:5

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kusema kile ambacho watu watasema pale ambapo wafalme wanatawala.

kwa maana miongoni mwenu yupo Mtakatiufu wa Israeli

"kwa sababu Mtakatifu wa Israeli, ambaye huishi miongoni mwenu, ana uwezo" au "kwa sababu Mtakatifu wa Israeli ana uwezo ana uwezo na anaishi miongoni mwenu"

Isaiah 13

Isaiah 13:1

kuhusu Babeli

Jina la mji lina maana ya watu wa Babeli. "kuhusu watu wa Babeli"

Amozi

Amozi alikuwa baba wa Isaya.

lia kwa sauti kwao

Neno "kwao" ina maana ya wanajeshi kutoka nchi nyingine.

malango ya waadilifu

Maana zaweza kuwa 1) "malango ya Babeli ambapo waadilifu wanaishi" au 2) "malango ya nyumba kubwa za waadilifu"

waadilifu

"watu wanaoheshimiwa" au "watawala"

watakatifu wangu

"wale ambao nimewaweka kando kwa ajili yangu" au "jeshii ambalo nimeliweka kando kwa ajili yangu"

Nmewaita wanamume wangu wenye uwezo kutekeleza hasira yangu

Kutekeleza hasira ya Mungu inawakilisha kuadhibu watu kwa sababu ya hasira ya Mungu. "Nimewaita wanajeshi wenye nguvu kuadhibu watu wa Babeli kwa sababu wamenikasirisha"

hata wanaoshangilia kwa kujisifu

"hata wale ambao wanashangilia kwa majivuno". Sababu ya wao kushangilia kwa majivuno inaweza kuwekwa wazi. "hata watu wangu ambao hushangilia kwa majivuno kwa sababu ya mambo makubwa nayofanya"

Isaiah 13:4

Kelele za kundi katika milima, kama watu wengi

Neno "kelele" linaeleweka. Misemo "kundi" na "watu wengi" ina maana moja. "kuna kelele ya watu wengi katika milima" au "Kuna kelele ya kundi kubwa la watu katika milima"

Kelele za ghasia ya falme kama mataifa mengi yaliyokusanyika pamoja

MaNeno "kuna" linaeleweka. Maneno "falme" na "mataifa" hapa yana maana ya jambo moja. "Kuna ghasia ya kelele ya falme nyingi zilizokusanyika pamoja"

anawakutanisha

"anawakusanya"

kutoka mbali juu ya upeo wa macho

"kutoka sehemu mbali kupita upeo wa macho" au "kutoka sehemu za mbali sana"

vyombo vyake vya hukumu

Wanajeshi ambao Mungu anawatuma kushambulia Babeli wanazungumziwa kana kwamba walikuwa silaha. "Hukumu" inawakilisha adhabu kwa sababu Mungu alihukumu Babeli. "'jeshi ambalo atalitumia kuadhibu Babeli"

Isaiah 13:6

Lia kwa kelele

"Paza sauti ya juu"

siku ya Yahwe ipo karibu

Jambo ambalo linatarajia kufanyika hivi karibuni linazungumziwa kana kwamba linakuja karibu. "siku ya Yahwe itatokea hivi karibuni"

inakuja na uhariibifu kutoka kwa Mwenyezi

Neno "inakuja" ina maana ya siku ya Yahwe. "Inakuja na uharibifu" ina maana uharibifu utatokea katika siku hiyo. "Uharibifu kutoka kwa Mwenyezi" ina maana ya kwamba Mwenyezi atawaangamiza. "katika siku hiyo, Mwenyezi Mungu atawaangamiza"

mikono yote huning'inia kwa ulegevu

Hii inaonyesha ya kwamba watu wote ni dhaifu sana na hawawezi kufanya jambo lolote.

kila moyo huyeyuka

Watu kuwa na hofu sana inazungumzwa kana kwamba mioyo yao huyeyuka. "kila mmoja anaogopa sana"

uchungu na maumivu utawakamata

Watu kujisikia maumivu mabaya ghafla na majonzi inazungumziwa kana kwamba maumivu na majonzi yalikuwa watu ambao huwakamata. "ghafla watahisi maumivu makubwa na uchungu"

kama mwanamke katika uchungu

Kuwa katika uchungu inawakilisha kuzaa mtoto. "kama mwanamke anayezaa mtoto" au "kama maumivu ya mwanamke ambaye anazaa mtoto"

nyuso zao zitawaka

Nyuso zao kuwa za moto na nyekundu inazungumziwa kana kwamba zilikuwa zikiungua. Sababu zinazowezekana za nyuso zao kuwa za moto ni 1) watu wanaogopa sana au 2) watu wanajisikia aibu au 3) watu wanalia. "nyuso zao zitakuwa za moto na nyekundu"

Isaiah 13:9

siku ya Yahwe inakuja kwa ghadhabu katili na hasira ya kumwagikia

Siku kuja kwa ghadhabu na hasira ina maana ya kwamba kutakuwa na ghadhabu na hasira katika siku hiyo. Nomino dhahania "ghadhabu" na "hasira" inaweza kuelezwa kwa vivumishi "ghadhabu" na "hasira". "katika siku ya Yahwe, atakuwa na ghadhabu na hasira sana"

hasira ya kumwagikia

Hasira hapa inazungumziwa kana kwamba yule ambaye ana hasira ni chombo kiliichojazwa na hasira. Hasira inayomwagikia ina maana ya kwamba ana hasira sana.

kufanya nchi kutiwa ukiwa

Hii inaweza kuandikwa upya ili kwamba nomino dhahania "tia ukiwa" inaelezwa kwa kitenzi "haribu". "kuharibu nchi"

Nyota za mbinguni na vilimia

"Nyota katika anga"

havitatoa mwanga wao

Kutoa mwanga inawakilisha "kung'aa". "haitang'aa"

Jua litafanywa kuwa giza

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe atauwekea giza jua" au "Jua litakuwa na giza"

Isaiah 13:11

Kauli Kiunganishi

Yahwe anaendelea kuzungumza juu ya kile atakachofanya katika siku ya Yahwe.

ulimwengu

Hii ina maana ya "watu wa ulimwengu"

waovu ... wanaojivuna ... wakatili

Misemo hii ina maana ya watu ambao wana sifa hizi. "watu waovu ... watu wanaojivuna ... watu wakatili"

wakatili

"watu wakatili"

na nitashusha chini kiburi cha wakatili

Kuwa chini mara nyingi inawakilisha kuwa mnyenyekevu. Kushusha kiburi cha watu chini inawakilisha kufanya wawe chini. "na nitawashuhsa wakatili"

Nitawafanya wanamume kuwa adimu kuliko dhahabu safi

Kwa nini kutakuwa na watu wachache sana inaweza kuwekwa wazi. "Nitasababisha watu wengi sana kufa mpaka watu wanaoishi watakuwa adimu zaidi kuliko dhahabu safi"

wanamume kuwa adimu kuliko dhahabu safi ... binadamu mgumu kumpata kuliko dhahabu safi ya Ofiri

Misemo hii miwili ina maana moja.

dhahabu safi ya Ofiri

Ofiri lilikuwa jina la sehemu ambapo kulikuwa na dhahabu safi.

Isaiah 13:13

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza.

Kama swala anayewindwa au kama kondoo asiyekuwa na mchungaji

"Kama swala ambaye hukimbia haraka pale watu wanapomwinda, na kama kondoo ambaye hana mchungaji anavyokimbia kutoka kwa wanyama pori"

swala

mnyama ambaye anafanana na mbawala. Watu huwawinda, na wanyama pori mara nyingine huwashambulia na kuwaua.

kama kondoo asiyekuwa na mchungaji

Kondoo ambao hawana mchungaji hawana mtu wa kuwalinda kutoka kwa wanyama pori ambao huwashambulia na kuwaua.

Isaiah 13:15

Yeyote atakayepatikana atauawa ... kila mmoja ambaye anakamatwa atakufa kwa upanga

Misemo hii miwili ina maana moja. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Adui ataua kwa upanga kila mtu anayempata"

Watoto wao wachanga pia watakatwa vipande

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Adui atawakata pia watoto wao wachanga katika vipande" au "Adui atawapiga watoto wao wachanga mpaka wafe"

mbele ya macho yao

"Mbele ya macho yao" ina maana ya "katika uwepo wao" au "huku wakitazama". Inaweza kuwekwa wazi ya kwamba wazazi hawakuw\vza kuwasaidia watoto wao wachanga. "huku wazazi wao wakitazama bila msaada"

Nyumba zao zitaporwa

Hii ina maana ya kwamba kila kitu chenye thamani kitaibiwa kutoka katika nyumba zao. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Adui atapora nyumba za watu" au "Adui ataiba kila kitu chenye thamani kutoka kwa nyumba za watu"

wake zao kubakwa

Hii ina maana ya kwamba maadui watashambulia wanawake na kuwalazimsha kufanya ngono pamoja nao. Maneno "watabakwa" yanaeleweka. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "wake zao watabakwa" au "maadui wao watawabaka wake zao"

Isaiah 13:17

Kauli Kiunganishi

Yahwe anaendelea kuzungumza.

Ninakaribia kuwatikisa Wamedi kuwashambulia

Kuwafanya watu kutaka kufanya kitu inazungumziwa kama kuwaamsha. "Ninataka kufanya Wamedi watake kuwashambulia"

Isaiah 13:19

Kauli Kiunganishi

Yahwe anaendelea kuzungumza.

falme zinazoshangaza zaidi

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "ufalme ambao watu hushangaa zaidi"

ufahari wa kiburi cha Wakaldayo

Nomino "kiburi" inaweza kuelezwa kwa kivumishi "kujivuna". "mji mzuri ambao Wakaldayo wanajivunia"

itapinduliwa

"itaangamizwa"

kama Sodoma na Gomora

"kama Sodoma na Gomora walivyopundiliwa".

haitakaliwa au kuishi kwake

Vitenzi hivi viwili vina maana moja. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Hakuna mtu ataishi ndani yake"

kwake kutoka kizazi mpaka kizazi

Msemo "kizazi mpaka kizazi" una maana ya vizazi vyote vya watu ambavyo vitaishi katika siku za usoni. "milele" "wakati wowote tena"

Mwarabu

Hii ina maana ya watu wa Kiarabu kwa ujumla, sio mtu mmoja. "Waarabu" au "watu wa Kiarabu"

Isaiah 13:21

Kauli Kiunganishi

Yahwe anaendelea kuzungumza kuhusu kile kitakachotokea kwa Babeli.

watalala pale

"watalala Babeli"

Nyumba zao

"'nyumba za watu"

bundi

Bundi ni ndege pori ambao huwinda usiku.

mbuni

Mbuni ni ndege pori wakubwa ambao hukimbia haraka na hawawezi kupaa.

Fisi

Fisi ni wanyama pori wakubwa ambao hufanana na mbwa na hula wanyama waliokufa. Sauti zao zaa juu husikika kama mtu achekavyo.

na mbweha katika kasri nzuri

Maneno "watalia" inaeleweka. "Na mbweha watalia ndani ya kasri nzuri"

mbweha

mbwa mwitu

Muda wake umekaribia, na siku zake hazitacheleweshwa

Misemo hii miwili ina maana moja. "Muda wake" na "siku zake" yote ina maana ya kipindi ambacho Mungu alichagua Babel kuangamizwa. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Kipindi ambacho yote haya yatatokea kwa watu wa Babeli kimekaribia, na hakuna kitu kitazuia"

Isaiah 14

Isaiah 14:1

Yahwe atakuwa na huruma kwa Yakobo

Hapa "Yakobo" ina maana ya vizazi vya Yakobo. "Yahwe atakuwa na huruma juu ya vizazi vya Yakobo"

kujishikiza katika nyumba ya Yakobo

Nyumba ya Yakobo ina maana ya vizazi vya Yakobo, Waisraeli. "jiunge na vizazi vya Yakobo"

Mataifa yatawaleta katika sehemu zao wenyewe

"Mataifa yatarudisha vizazi vya Yakobo katika nchi ya Israeli"

nyumba ya Israeli

Hii ina maana ya Waisraeli, vizazi vya Israeli. "vizazi vya Israeli"

Watachukua mateka wale ambao waliwakamata

"Wanajeshi wa Israeli watachukua kama mateka wale ambao waliwakamata Waisraeli"

Isaiah 14:3

kutoka katika mateso yako na maumivu makali

Neno "yako" ni umoja, lakini lina maana ya watu wa Israeli. Pia, "mateso" na "maumivu makali" ina maana moja na inatumika pamoja kwa msisitizo. "kutoka kwa vitu ambavyo uliteseka navyo sana"

Jinsi mkandamizaji alivyofikia mwishoni

"Mkandamizaji amefikia mwisho". Hii ni hali ya mshangao.

ghadhabu ya wenye kiburi ikaisha

Maneno "jinsi" na "umeisha" inaeleweka. "jinsi ghadhabu ya wenye kiburi imefika mwisho" au "kiburi na ghadhabu yake imekamilika"

ghadhabu ya wenye kiburi ikaisha

"ghadhabu ya wenye kiburi" ina maana ya mfalme wa Babeli kuwa na kiburi na kuwatendea mataifa mengine ukatili. "ukatili wake umefikia mwisho" au "hawezi tena kukandamiza watu"

Isaiah 14:5

Kauli Kiunganishi

Hii ni sehemu ya wimbo wa dhihaki ambao Waisraeli wataimba kwa mfalme wa Babeli.

Yahwe amevunja gongo la waovu

Gongo la waovu huenda lina maana ya kijiti ambacho watu waovu wangepigia watu wengine. Kuvunja kijiti hicho inawakilisha kuangamiza nguvu yao ya kufanyia watu ukatili. "'Yahwe ameangamiza nguvu ya waovu"

fimbo ya kifalme ya hao watawala

Fimbo ya kifalme inawakilisha nguvu ya mtawala kutawala. Kuvunja fimbo ya kifalme inawakilisha kuangamiza nguvu ya watawala. "Yahwe ameangamiza nguvu ya watawala waovu"

iliyowapiga watu

"ambaye aliwapiga watu". Watu waovu walipiga watu kwa gongo lao.

kwa mapigo yasiyokoma

"bila kukoma" au "tena na tena"

iliyotawala mataifa

"ambaye alishinda mataifa mengine"

kwa shaambulio ambalo halikuzuilika

"kuwashambulia bila kuacha"

Isaiah 14:7

Kauli Kiunganishi

Hii ni sehemu ya wimbo wa dhihaki ambao Waisraeli wataimba kwa mfalme wa Babeli.

Dunia nzima

Hii ina maana ya kila mtu duniani. "kila mtu juu ya dunia"

Hata mti wa mvinje unashangilia juu yako pamoja na mierezi ya Lebanoni

Isaya anazungumzia miti kana kwamba ilikuwa watu ambao wanaweza kushangilia. Hii inasisitiza ya kwamba ni jambo kubwa ya kwamba Mungu amezuia mfalme wa Babeli hadi asili inashangilia kama ingeweza. "Itakuwa kana kwamba hata miti ya mvinje na mierezi ya Lebanoni hushangilia juu yako"

unashangilia juu yako

Kwa nini wanashangilia inaweza kuwekwa wazi. "furahia ya kwamba Mungu amekufanya bila nguvu"

Kwa maana umelazwa chini

Kulazwa chini inawakilisha kufanywa bila nguvu na kutokuwa na umuhimu. "Kwa kuwa umekuwa bila nguvu"

Kuzimu chini pana shauku ya kukutana na wewe

Kuzimu inazungumziwa kana kwamba ilikuwa mtu ambaye ana shauku ya kukutana na wageni wake. Hii inadokeza ya kwamba mfalme amekufa. "Kuzimu ni kama mwenyeji mwenye shauku ya kukutana nawe"

Inaamsha wafu kwa ajili yako, wafalme wote wa dunia

"Inaamsha wafu kwa ajili yako, wafalme wote wa dunia". Kuzimu inazungumzia kana kwamba ilkuwa mtu ambaye anaweza kumsha wale ambao wamo ndani yake". "Wafalme wote waliokufa wa dunia wa kuzimu huamka kukusalimia"

Isaiah 14:10

Kauli Kiunganishi

Hii ni sehemu ya wimbo wa dhihaki ambao Waisraeli wataimba kwa mfalme wa Babeli. Hapa wanaimba juu ya wafalme waliokufa wa kuzimu watakavyosema kwake.

Wote watazungumza na kusema kwako

Neno "wata" lina maana ya wafalme waliokufa wa kuzimu, na neno "kwako" lina maana ya mfalme wa Babeli.

Ufahari wako umeletwa chini mpaka kuzimu

Wafalme waliokufa watazungumza na mfalme wa Babeli kutokuwa na ufahari tena kana kwamba ufahari wake umeshuka chini kuzimu. "Ufahari wako umekwisha pale Mungu alipokutuma hapa kuzimu"

kwa sauti ya nyuzi za vinanda

Watu walifanya muziki kwa njuzi za vinanda kumheshimu mfalme. Wafalme waliokufa hawatawazungumzia watu tena kuheshimi mfalme wa Babeli kwa muziki kana kwamba muziki ulikwenda kuzimu. "pamoja na sauti ya watu wakicheza muziki kukuheshimu"

Funza wanasambazwa chini yako

Funza chini ya mwili wake uliokufa inazungumziwa kana kwamba zilikuwa kitanda. "Unalala juu ya kitanda cha funza" au "Unalala ju funza wengi"

funza hukufunika

Funza katika mwili wake wote inazungumziwa kana kwamba walikuwa wakimfunika kama blangeti. "Funza wanakufunika kama blangeti" au "Kuna funza ju ya mwili wako wote"

Isaiah 14:12

Kauli Kiunganishi

Hii ni sehemu ya wimbo wa dhihaki ambao Waisraeli wataimba kwa mfalme wa Babeli.

Jinsi ulivyonguka kutoka mbinguni, nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi

Nyota ya alfajiri ni nyota inayong'aa ambayo inainuka kabla tu ya asubuhi. Watu wa Israeli watamchukulia mfalme wa Babeli kwa msemo wa hii nyota ili kuonyesha ya kwamba aliwahi kuwa mkuu, lakini sasa hayupo. "Ulikuwa kama nyota inayong'aa ya asubuhi, lakini umeanguka kutoka angani"

Jinsi ulivyokatwa chini ardhini

Watu wa Israeli watazungumzia mfalme wa Babeli kana kwamba alikuwa mti ambao ulikuwa ulikatwa chini. "Umeshindwa kama mti ambao mtu ameukata chini ardhini"

Nitakaa juu ya mlima wa kusanyiko

Hii inagusia kisasili ya kwamba watu wengi katika Mshariki ya Karibu ya Zamani, miungu wa Wakaanani walikutana baraza juu ya mlima katiika sehemu ya kaskazini ya Ashuru. Kukaa juu ya mlima inawakilisha kutawala kwa miungu. "Nitatawala juu ya mlima ambao miungu hukusanyka"

katika mipaka ya mbali ya kaskazini

"katika sehemu za kusni zaidi"

Isaiah 14:15

Kauli Kiunganishi

Hii ni sehemu ya wimbo wa dhihaki ambao Waisraeli wataimba kwa mfalme wa Babeli.

Ingawa sasa unaletwa chini kuzimu

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Lakini sasa Mungu amekutuma chini mpaka kuzimu"

Je! huyu ni mtu

Watu watatumia swali hili aidha kumdhihaki mfalme wa Babeli, au kuonyesha mshangao wao ya kile kilichotokea kwake. "Hakika, huyu siye mwanamume"

aliyefanya dunia kutetemeka

Maana zaweza kuwa 1) dunia inatetemeka jeshi la mfalme lilipotembea kuwashinda watu, au 2) hii ina maana ya watu wa dunia kutetemeka kwa hofu juu yake.

kutikisa falme

Maana zaweza kuwa 1) hii sitiari kwa ajili ya "falme zilizodhindwa" au 2) huu ni mfano wa maneno kwa ajili ya "alitisha watu wa falme".

aliyeifanya dunia kama nyika

"ambaye alifanya maeneo ambao watu waliishi kuwa nyika"

Isaiah 14:18

Kauli Kiunganishi

Huu ni mwisho wa wimbo wa dhihaka ambao Waisraeli wataimba kwa mfalme wa Babeli.

wote watalala chini kwa heshima

Hii ina maana ya kwamba miili yao itazikwa kwa naman ya heshima. "wafalme wote ambao wamekufa wanazikwa kwa namna ya heshima"

Lakini umerushwa nje ya kaburi lako

Kurushwa nje ya kaburi inawakilisha kutozikwa. "lakini haujazikwa. Mwili wako umeachwa juu ya ardhi"

kama tawi lililotupwa

Tawi lilitupwa linawakilisha kitu kisichokuwa na thamani. "kama tawi lisilo na thamani ambalo hutupwa kando"

wafu wamekufunika kama vazi

Hii inawakilisha maiti nyingi kuwa juu ya mwili wake. "Miili ya wafu inafunika kabisa mwili wako" au "Miili ya wanajeshi waliokufa imerundikwa juu ya mwili wako"

wale waliochomwa kwa upanga

Hii inaelezea "wafu" ni kina nani katika mwanzo wa sentensi. Kuchomwa na upanga inawakilisha kuuliwa vitani. "wale ambao waliuliwa vitani"

wanaoshuka chini katika mawe ya shimo

Shimo lina maana aidha ya jehanamu, au shimo kubwa katika ardhi ambapo miili mingi ya wafu inatupwa.

Hautajiunga nao katika kuzikwa

Neno "nao" lina maana ya wafalme wengine ambao walikufa na kuzikwa vizuri. Kuwaunga katika kuzikwa inawakilisha kuzikwa kama wao. "hautazikwa kama wafalme wengine walivyozikwa"

Watoto wa waovu hawatatajwa tena

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "hakuna mtu atayezungumza tena kuhusu uzao wa waovu"

Isaiah 14:21

Andaa machinjio yako kwa ajili ya watoto wake

Hii inaweza kuandikwa ili kwamba nomino dhahania "machinjio" ilelezwa kwa kitenzi "ua"."Jiandae kuwaua watoto wa mfalme wa Babeli"

kwa maana udhalimu wa mababu zao

Hii inaweza kuandikwa ili kwamba nomino dhahania "udhalimu" inaelezwa kama kitenzi "tenda dhambi sana". "kwa sababu babu zao walitenda dhambi sana"

ili wasiweze kuinuka juu

Hapa "kuinuka juu" inawakilisha aidha kuwa na nguvu au kushambulia. "ili wasiweze kuwa na nguvu" au "ili wasishambulie"

kumiliki dunia

Hii inawakilisha kutawala juu ya watu wa dunia, katika suala hili kwa kuwashinda wao. "tawala juu ya watu wa dunia" au "washinde watu wa dunia"

na kuijaza dunia nzima kwa miji

Hii inawakilisha kusababisha dunia kuwa na mijij mingi. "na kujenga miji duniani kote"

Nitainuka juu dhidi yao

Hii ina maana ya kwamba Mungu atafanya jambo dhidi yao. neno "yao" lina maana ya watu wa Babeli. "Nitawashambulia" au "Nitatuma watu kuwashambulia"

hili ni tamko la Yahwe wa majeshi

Hii inaweza kuandikwa ili kwamba nomino dhahania "tamko" lielezwa kama kitenzi "tamka" au "sema kwa dhati". "hivi ndivyo Yahwe wa majeshi alivyotamka" au "hivi ndivyo kile Yahwe wa majeshi alivyosema kwa dhati"

Yahwe wa majeshi

Yahwe wa majeshi wa Israeli.

Nitakata jina la Babeli, uzao, na watoto

"Kukata" inawakilisha kuangamiza. Hapa "Babeli" ina maana ya watu wa Babeli. Pia, "jina" ina maana ya aidha umaarufu wa Babeli au Babeli yenyewe kama ufalme. "Nitaangamiza Babeli, pamoja na watoto wa watu na wajukuu"

Pia nitaifanya

Neno "nitaifanya" ina maana ya mji wa Babeli. Miji mara kwa mara ilizungumziwa kana kwamba ilikuwa wanawake. "Pia nitaifanya"

milki ya bundi

Hii inawakilisha wanyama pori wanaoishi katika mji kwa sababu hakuna watu pale. "sehemu ambayo bundi huishi" au "sehemu ambayo wanyma pori huishi"

na kuwa dimbwi za maji

Kusababisha kuwepo vinamasi au madimbwi ya maji yaliyotulia ambapo mji ulikuwepo inazungumziwa kama kufanya mji kuwa vitu hivyo. "na katika sehemu ambapo kuna madimbwi yaliyotulia"

nitaifagia kwa ufagio wa uharibifu

Hii inawakilisha kuangamiza Babeli kabisa na kuifanya isiwepo tena kana kwamba ilikuwa uchafu usiokuwa na thamani ambao watu hufagia. "Nitaangamiza kabisa, kama kufagia kwa ufagio"

Isaiah 14:24

Yahwe wa majeshi

Yahwe wa majeshi ya Israeli

kama nilivyodhamiria, ndivyo itakavyokua; na kama nilivyokususida, basi ndivyo itakuwa

Misemo hii miwili ina maana moja. "vitu ambavyo nimepanga hakika vitatimia"

nitavunja Ashuru katika nchi yangu

Kuvunja inawakilisha kushinda. "Nitashinda Ashuru katika nchi yangu" au "Nitasababisha Ashuru katika nchi yangu kushindwa"

Ashuru

Hii inawakilisha mfalme wa Ashuru na jeshi lake. "mfalme wa Ashuru na jeshi lake" au "jeshi la Ashuru"

kumkanyaga chini ya mguu

Hii inawakilisha kumshinda kabisa

Kisha nira yake itainuliwa kutoka kwao na mzigo wake kutoka katika bega lao

Hii inaweza kuelezwa kwa kitenzi cha kutenda. "Kisha nitainua nira yake kutoka kwao na mzigowake kutoka katika bega lao"

Kisha nira yake itainuliwa kutoka kwao na mzigo wake kutoka katika bega lao

Misemo hii miwili ina maana moja. Kuinua nira na mzigo inawakilisha kuwaweka watu huru katika utumwa. "Kisha nitawaweka Waisraeli huru kutoka katikautumwa wa Ashuru kama kutoa mzigo mzito kutoka katika mabega yao"

nira yake ... mzigo wake

Neno "yake" ina maana ya Ashuru.

kutoka kwao ... kutoka katika bega lao

Maneno "kwao" na "lao" ina maana ya watu wa Israeli.

Isaiah 14:26

Taarifa ya Jumla

Huyu anaweza kuwa Isaya akizungumza au inaweza kuwa Yahwe akizungumza.

Huu ni mpango ambao umekususdiwa kwa ajili ya dunia nzima

Wazo la "umekusudiwa" linaweza kuelezwa kwa kitenzi cha kutenda."Hu ni mpango ambao Mungu anakududia kwa ajili ya dunia nzima"

na huu ndio mkono ambao umeinuliwa juu ya mataifa yote

Mungu kuwa tayari kuadhibu mataifa inazungumziwa kana kwamba aliinua mkono wake ili kuwapiga. Neno "mkono" unaweza kuwakilisha nguvu yake. "na hii ndiyo nguvu ya Yahwe kuadhibu mataifa yote" au "hivi ndivyo Yahwe atakavyoadhibu mataifa"

ni nani atakayemzuia?

Swali hili linasisitiza ya kwamba hakuna mtu wa kumzuia Yahwe. "hakuna mtu ambaye anaweza kumzuia"

Yahwe wa majeshi

Yahwe wa majeshi ya Israeli.

mkono wake umeinuliwa

Hii inawakilisha Yahwe kuwa tayari kuadhibu mataifa. "Yupo tayari kuwaadhibu"

ni nani atakayeurudhisha?

Swali hili linatumika kusema ya kwamba hakuna mtu anayeweza kugeuza mkono wa Yahwe. Kugeuza mkono wake inawakilisha kumzuia kuadhibu mataifa.

Isaiah 14:28

rungu iliyokupiga imevunjika

Rungu ambayo ilimpiga Filisti inawakilisha mfalme aliyetuma jeshi lake kuwashambulia. Kuvunjika inawakilisha aidha kufa au kushindwa. "mfalme aliyetuma jeshi lake dhidi yako amekufa" au "jeshi ambalo lilikushambulia limeshindwa"

Kwa maana katika mzizi wa nyoka kutaota kifutu ... mtoto wake atakuwa nyoka mkali anayepaa

Misemo hii miwili yote ni taswira ya mtoto wa nyoka kuwa na madhara zaidi ya nyoka. Inawakilisha mrithi wa mfalme kuwa na nguvu zaidi na katili kuliko mfalme wa kwanza.

kifutu

aina ya nyoka mwenye sumu

nyoka mkali anayepaa

Hapa neno "kali" huenda ina maana ya kung'atwa na sumu ya nyoka, na neno "kupaa" ina maana ya kusogea kwake kwa haraka. "nyoka mwenye sumu anayesogea kwa haraka"

mzaliwa wa kwanza wa maskini

Hii inawakilisha maskini zaidi wa watu. "Maskini zaidi wa watu" au "maskini zaidi wa watu wangu"

Nitaua mzizi wako kwa njaa ambaye itawaua wote waliopona wa kwako

Hapa "mzizi wako" ina maana ya watu wa Filisti. "Nitawaua watu wako kwa njaa ambayo itawaua wote waliopona wa kwako"

Isaiah 14:31

Vuma, lango; lia, mji

Hapa "lango" na "mji" inawakilisha watu katika malango ya mji katika miji. "Vuma, enyi watu katika malango ya mji; lieni, nyie watu katika miji"

utayeyuka mbali

Kuyeyuka inawakilisha kuwa dhaifu kwa sababu ya uoga. "utakuwa dhaifi kwa uoga"

Kwa maana katika kaskazini linakuja wingu la moshi

Hii inadokeza ya kwamba jeshi kubwa linakuja kutoka kaskazini. "Kwa maana kutoka kaskazini linakuja jeshi kubwa pamoja na wingu la moshi"

wingu la moshi

Maana zaweza kuwa 1) hii inawakilisha wingu la vumbi ambalo jeshi hutengeneza wanaposafiri katika njia za vumbi. "wingu la vumbi" au 2) kuna moshi mwingi kwa sababu ya vitu vyote ambavyo jeshi linaangamiza na kuchoma. "moshi mwingi"

hakuna mchelewaji katika safu zake

"hakuna aliye katika safu zake anayetembea poole pole nyuma ya wenzake"

Je! mtu atajibu nini kwa wajumbe wa taifa hilo?

Mwandishi anatumia swali hili kutambulisha maagizo yake juu ya jinsi Waisraeli wanatakiwa kuzungumza kwa wajumbe. "Hivi ndivyo tutakavyojibu wajumbe wa Filisti"

Yahwe ameianzisha Sayuni

"Yahwe alianzisha Sayuni"

na ndani mwake

"na Yerusalemu" au "kule"

walioteseka wa watu wake

"wale watu wake ambao walikuwa wameteswa"

Isaiah 15

Isaiah 15:1

Taarifa ya Jumla

Mara kwa mara katika unabii, matukio yajayo yanaelezwa kama yanatokea sasa au katika kipindi cha nyuma. Hii inasisitiza ya kwamba tukio hakika litatokea.

Tamko

"Hiki ni kile ambacho Yahwe anatamka" au "Huu ni ujumbe utokao kwa Yahwe"

Ari ... Kiri ... Diboni ... Nebo ... Medeba

Haya ni majina na miji ya Moabu.

Ari ya Moabu imewekwa kama takataka na kuangamizwa

Maneno "imewekwa kama takataka" na "kuangamizwa" ina maana moja na inasisitiza ya kwamba mji uliharibiwa kabisa. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Majeshi ya adui yataangamiza kabisa Ari ya Moabu"

kwenda juu kileleni kulia

Hapa "juu kileleni" ina maana ya katika hekalu au dhabahu ambalo limejengwa juu ya nchi kama kilima au upande wa mlima. "kwenda juu hekaluni juu ya juu ya kilima kulia"

Moabu huomboleza juu ya Nebo na juu ya Madeba

Majina ya sehemu hizi ina maana ya watu wanaoishi kule. "watu wa Moabu watalia kwa sababu ya kile kilichotokea kwa miji ya Nebo na Medeba"

Vichwa vyao vyote vimenyolewa wazi na ndevu zao zote zimekatwa

Wanafanya hivi kuonyesha huzuni yao kuu. "Wote watanyoa vichwa vyao na kukata ndevu zao na kuhuzunika"

Isaiah 15:3

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza unabii kuhusu watu wa Moabu. Mungu anafafanua matukio ambayo yatatokea wakati ujao kana kwamba inatokea katika wakati wa sasa.

wanavaa nguo ya gunia

Wanafanya hivi kuonyesha huzuni yao kuu. "wanavaa nguo za gunia na kuomboleza"

Heshboni ... Eleale ...Yahasa

Haya ni majina ya miji mikubwa na miji midogo.

Heshboni na Eleale zikapaza sauti

Majina ya miji hii inawakilisha watu wa miji hii. "Watu wa Hebroni na Eleale wanapaza sauti"

wanatetemeka kati yao

Kutetemeka kimwili ni dalili ya hofu. "watakuwa wamejazwa kabisa kwa hofu"

Isaiah 15:5

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza unabii kuhusu watu wa Moabu. Mungu anafafanua matukio ambayo yatatokea katika muda ujao kana kwamba yanatokea katika wakati wa sasa.

Moyo wangu unalia kwa ajili ya Moabu

Moyo unawakilisha hisia. Mungu anazungumzia huzuni yake kubwa kana kwamba moyo wake ulilia kwa sauti. "Nina huzuni sana juu kile kinachoendelea Moabu"

wakimbizi wake hutoroka

"wakimbizi kutoka Moabu watatoroka". Mkimbizi ni mtu ambaye hutoroka ili kwamba adui zake wasiweze kumkamata.

Soari ... Eglathi Shelishiya ... Luhithi ... Horonaimu ... Nimrimu

Haya ni majina ya miji mikubwa na miji midogo.

juu ya uharibifu

Hii inaweza kuelezwa ili kwamba nomino dhahania "uharibifu" inaelezwa kama kitenzi "kuangamizwa". "kwa sababu mji wao umeangamizwa"

wingi

"Kila kitu"

kijito cha mipopla

Hii inaweza kumaanisha mto katika mpaka wa kusini wa Moabu.

Isaiah 15:8

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza unabii kuhusu watu wa Moabu. Mungu anafafanua matukio ambayo yatatokea katika muda ujao kana kwamba inatokea katika muda wa sasa.

Kilio kimeenda kuzunguka eneo la Moabu

Watu kulia na wengine kusikia inazungumziwa kana kwamba kilio kimetoka nje. "Watu juu ya eneo lote la Moabu wanalia"

maombolezo yamefika mbali mpaka Eglaimu na Beer-Elimu

Maneno "yamefika" yanaeleweka. Watu kulia na wengine kusikia inazungumzwa kana kwamba kilio kimetoka na kufika mbali hadi maeneo haya mawili. "kilio kimefika mbali mpaka Eglaimu na Beer-Elimu" au "watu hata umbali wa Elaimu na Beer-Elimu wanalia"

Eglaimu ... Beer-Elimu ... Dimoni

Haya ni majina ya miji mikubwa na miji midogo. Dimoni ulikuwa mji mkuu wa nchi ya Moabu. Baadhi ya tafsiri za kisasa zina "Diboni" badala ya "Dimoni".

lakini nitaleta zaidi juu ya Dimoni

Hapa "nitaleta" ina maana ya Yahwe. Pia, "juu ya Dimoni" ina maana ya watu. "lakini nitasababisha hata matatizo zaidi kwa watu wa Dimoni"

Isaiah 16

Isaiah 16:1

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza unabii kuhusu watu wa Moabu. Mungu anaelezea matukio yatakayotokea katika siku za usoni kana kwamba yanatokea wakati wa sasa. Mstari wa kwanza huenda ndicho Mungu anasema watawala wa Moabu watasema kwao wenyewe.

Tuma kondoo dume kwa mtawala wa nchi

Wamoabu watatuma kondoo dume kwa mfalme wa Yuda ili kwamba aweze kuwalinda kutoka kwa jeshi la adui.

Sela

Hili ni jina la mji.

binti Sayuni

"binti" wa mji ina maana ya watu wa mji. "Watu wa Sayuni" au "Watu wanaoishi Sayuni"

Kama ndege wanaozurura, kama kiota kilivyosambaa, kwa hiyo wanawake wa Moabu watakuwa katika vivuko vya Mto Arnoni

Watu wote wa Moabu, ambayo inajumlisha wanawake, wanalazimishwa kutoroka kutoka kwenye nyumba zao. "Kama ndege wasio na nyumba, wanawake wa Moabu watatoroka kupitia mto hadi nchi nyingine"

Kama ndege wanaozurura, kama kiota kilivyosambaa

Misemo hii miwili kimsingi ina maana moja.

Isaiah 16:3

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza unabii kuhusu watu wa Moabu. Mungu anafafanua matukio ambayo yatatokea katika siku za usoni kana kwamba yatatokea wakati wa sasa. Mistari ya 3 na 4 huenda ni ujumbe ambao watawala wa Moabu hutuma kwa mfalme wa Yuda.

toa kivuli kama usiku katikati ya siku

Joto la katikati ya siku linawakilisha mateso ya Wamoabu kutoka kwa adui zao, na kivuli kinawakilisha ulinzi kutoka kwa maadui wao. Kufafanisha kivuli na usiku inaonyesha ya kwamba wanataka ulinzi imara. "tulinde kikamilifu kutoka kwa adui zetu kama kivuli kikubwa kinavyolinda watu kutoka na jua kali"

Waruhusu waishi miongoni mwenu, wakimbizi kutoka Moabu

"Ruhusu wakimbizi kutoka Moabu kuishi pamoja nawe". Hapa "mwenu" ina maana ya watu wa Yuda.

uwe sehemu ya maficho kwa ajili yao kutoka kwa mharibifu

Kutoa sehemu ya maficho inazungumziwa kama kuwa sehemu ya kujificha. "wapatie sehemu ya kujificha kutoka kwa wale ambao wanajaribu kuwaangamiza" au "wafiche kutoka kwa wale wanaotaka kuwaangamiza"

Isaiah 16:5

ufalme utaimarishwa katika agano la uaminifu

Hapa "ufalme" una maana ya nguvu ya kutawala kama mfalme. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Yahwe atakuwa mwaminifu kwa agano na atamteua mfalme"

na mmoja kutoka katika hema la Daudi atakaa pale kwa uaminifu

Hapa "hema la Daudi" inawakilisha familia ya Daudi, ikijumlisha uzao wake. Kukaa juu ya kiti cha enzi inawakilihsa kutawala. "na uzao wa Daudi utatawala kwa uaminifu"

atakapotafuta haki

Kutafuta haki inawakilisha kutaka kufanya kile ambacho ni haki.

Isaiah 16:6

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza unabii kuhusu watu wa Moabu. Mungu anafafanua matukio ambayo yatatokea katika siku za usini kana kwamba yanatokea katika wakati wa sasa.

Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu, majivuni yake, kujidai kwake, na hasira yake

Maneno haya "cha Moabu" na "yake" yana maana ya watu wa Moabu. "Tumesikia ya kwamba watu wa Moabu wana kiburi na majivuni, wanajidai na wana hasira"

Tumesikia

Maana zaweza kuwa 1) Isaya anazungumza na "Tumesikia" ina maana ya kwake na watu wa Yuda, au 2) Mungu anazungumza na "Tumesikia" ina maana ya Mungu.

Lakini kuringa kwake ni maneno matupu

"Lakini kile wanachosema kuhusu wao haina maana yoyote" au "Lakini kile wanachojidai nacho sio cha kweli"

Kwa hiyo Moabu anaomboleza kwa ajili ya Moabu - wote wanaomboleza

"Moabu" inawakilisha watu wa Moabu. "Kwa hiyo watu wa Moabu watalia kwa sauti juu ya kile kilichotokea kwa miji yao"

kwa maana keki ya zabibu kavu ya Kir-Haresethi

"kwa sababu hakuna keki za zabibu kavu katika Kir-Haresethi"

keki ya zabibu kavu

Neno la Kiebrania linalotumiwa hapa lina maana aidha ya "keki ya zabibu kavu" au "wanamume".

Kir-Haresethi

"Kir-Haresethi" ni jina la mji.

Isaiah 16:8

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza unabii kuhusu watu wa Moabu. Mungu anafafanua matukio ambayo yatatokea katika siku za usoni kana kwamba zilitokea katika kipindi cha nyuma.

Heshboni

Haya ni majina ya miji mikubwa na miji midogo.

Sibma ... Yazeri

Haya ni majina ya miji.

Watawala wa mataifa wamekanyaga mizabibu iliyo bora

Nchi ya Moabu ilijulikana kwa mashamba yake ya mizabibu. Hapa Mungu anafafanua nchi ya Moabu kama shamba moja kubwa la mizabibu. Hii inasisitiza ya kwamba watawala, ambao ina maanisha majeshi, waliangamiza kabisa kila kitu ndani ya Moabu.

Isaiah 16:9

Taarifaya Jumla

Hii inaendeleza kufafanua nchi ya Moabu kama shamba kubwa la mizabibu. Mungu anaelezea matukio yatakayotokea katika siku za usoni kana kwamba yanatokea katika wakati wa sasa.

Hasa nitalia

Katika 16:9-10 neno "nitalia" lina maana ya Yahwe.

nitakumwagilia kwa machozi yangu

Mungu anazungumza kuhusu majonzi yake kwa miji hii kana kwamba angelia sana na machozi yake mengi yataanguka juu yao. "Nitalia sana juu yako"

Yazeri ... Sibma

Haya ni majina ya miji

Heshboni ... Eleale

Haya ni majina ya miji mikubwa na miji midogo.

Kwa maana katika mashamba yako ya matunda ya kipindi cha joto na mavuno nimemaliza keleleza shangwe

"kelele za shangwe" zinawakilisha watu kupiga kelele za shangwe juu ya mavuno ya matunda ya miti. "Kwa sababu ya kile nitakachofanya, hautapiga kelele tena ya shangwe utakapovuna mashamba yako ya matunda ya kipindi cha joto"

Nimeweka mwisho kelele za yule ambaye hukanyaga

Hapa "kelele" ina maana ya furaha ya watu wanaokanyaga mizabibu kutengeneza divai. "kwa hiyo watu wanaokanyaga mizabibu hawapigi kelele za furaha"

Isaiah 16:11

Taarifa ya Jumla

Hiiinaendeleza unabii kuhusu watu wa Moabu. Mungu anafafanua matukio ambayo yatatokea katika siku za usoni kana kwamba yanatokea kipindi cha sasa.

Kwa hiyo moyo wangu unashuhsa pumzi kama kinubi cha Moabu

Msemo "moyo wangu" unawakilisha Yahwe na hisia zake za huzuni. Analinganisha kushusha pumzi kama sauti ya wimbo wa huzuni unaochezwa katika kinubi. "Kwa hiyo ninashusha pumzi kama wimbo wa huzuni katika kinubi"

Moabu .. mwenyewe ... lake

Maneno haya yote yana maana ya watu wa Moabu.

kiumbe changu cha ndani kwa ajili ya Kir-Haresethi

Msemo "kiumbe changu cha ndani" inawakilisha Yahwe. Neno "kushusha pumzi" linaeleweka kutoka kwa msemo uliopita. "kiumbe changu cha ndani kwa ajili ya Kir-Haresethi" au "Nina huzuni sana kwa ajili ya watu wa Kir-haresethi"

maombi yake hatatimiza kitu

"maombi yake hayatajibiwa"

Isaiah 16:13

Hili ni neno

"Huu ni ujumbe". Hii ina maana ya kile kilichosemwa katika 15:1-16:12

kuhusu Moabu

Neno "Moabu" lina maana ya watu wa Moabu.

utukufu wa Moabu utatoweka

"Nchi ya Moabu haitakuwa na utukufu tena"

Isaiah 17

Isaiah 17:1

kuhusu Dameski

Dameski ni jina la mji.

miji ya Aroeri itatelekezwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Watu wote watatelekeza miji ya Aroeri"

hakuna atakayewatisha

Neno "atakayewatisha" ina maana ya kondoo

Miji iliyoimarishwa itatoweka kutoka Efraimu

Efraimu ilikuwa kabila kubwa zaidi la Israeli. hapa linawakilisha ufalme wote wa kaskazini wa Israeli. "Miji imara itatoweka kutoka Israeli"

itatoweka

Hii haimaanishi ya kwamba zitapotelea, lakini miji ile itaangamizwa.

ufalme wa Dameski

Maneno "itatoweka" inaeleweka kutoka kwa msemo uliopita. Dameski ilikuwa mahali ambapo mfalme wa Aramu alitawala. Ufalme kutoweka unawakilisha mflame kutokuwa tena na nguvu za kifalme. "ufalme utatoweka kutoka Dameski" au "hapatakuwa na nguvu ya kifalme Dameski"

Aramu

Aramu ni jina la taifa.

watakuwa kama utukufu wa watu wa Israeli

Kwa kuwa watu wa Israeli hawakuwa na utukufu tena, hii ilimaanihsa ya kwamba waliosalia wa Aramu hawatakuwa na utukufu tena. "hawatakuwa na utukufu tena, kama watu wa Israeli" au "Nitaleta aibu juu yao kama nilivyofanya kwa watu wa Israeli"

tamko la Yahwe wa majeshi

Hii inaweza kuandikwa upya ili kwamba nomino dhahania "tamko" ielezwe kama kitenzi "alitamka" au "alisema kwa dhati". "Hivi ndivyo Yahwe wa majeshi alivyotamka" au "hivi ndivyo Yahwe wa majeshi alivyosema kwa dhati".

Isaiah 17:4

Itakuja kuwa

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya tukio muhimu ambalo litatokea.

utukufu wa yakobo utakuwa mwembamba, na unene wa mwili wake utadhoofika

Hapa "Yakobo" ina maana ya ufalme wa Israeli. Israeli hatakuwa na utukufu tena. Ila atakuwa dhaifu na maskini.

itakuwa kama pale ambapo wavunaji walikusanya nafaka iliyosimama ... katika bonde la Warefai

Hakutakuwa na kitu kinachobaki katika nchi baada ya Mungu kuadhibu watu wa Israeli.

bonde la Warefai

Hili ni bonde ambapo watu kawaida kuotesha na kuvuna chakula kingi.

Isaiah 17:6

Taarifa ya Jumla

Hii inaendelea kulinganisha taifa la Israeli na shamba baada ya kuvunwa.

Masazo ya mavuno yatabaki

Neno "masazo ya mavuno" hapa yanawakilisha watu ambao bado wanaishi Israeli. "Lakini kutakuwa na watu wachache waliosalia Israeli"

kama pale mzeituni unapotikiswa

Watu walivuna mizeituni kwa kutikisa ili kwamba matunda yaweze kudondoka. "kama matunda machache ambayo yanabaki juu ya mizeituni baada ya watu kuivuna"

manne au matano

Neno "matunda" linaeleweka kutoka kwa msemo kabla ya huu. "matunda manne au matano"

hili ni tamko la Yahwe

Hii inaweza kuandikwa upya ili kwamba nomino dhahania "tamko" ielezwe kama kitenzi "alitamka" au "alisema kwa dhati". "Hivi ndivyo Yahwe wa majeshi alivyotamka" au "hivi ndivyo Yahwe wa majeshi alivyosema kwa dhati".

wanamume watamtazama kuelekea Muumba wao ... watamtazama Mtakatifu wa Israeli

Kutazama kuelekea Mungu hapa inawakilisha kuwa na tumaini kuwa atawasaidia. "wanamume watakuwa na tumaini ya kwamba Muumba wao, Mtakatifu wa Israeli, atawasaidia"

wanamume watamtazama

Neno "wanamume" linawakilisha watu kwa ujumla. "watu watamtazama"

macho yao yatatazama

Hapa "macho" yanawakilisha watu ambao wanatazama. "watatazama" au"watu watatazama"

Mtakatifu wa Israeli

Mtakatifu wa Israeli.

Isaiah 17:8

Hawataangalia katika madhabahu

Kutazama madhabahu kunawakilisha kuabudu sanama kwa tumaini ya kwamba sanamu zitawasaidia. "hawataabudu sanamu katika madhabahu yao" au "Watu wa Israeli hawatakwenda katika madhabahu yao na kuuliza sanamu zao kuwasaidia"

kazi ya mikono yao

Kuzungumzia mikono hapa inasisitiza ya kwamba watu walitengeneza madhabahu au sanamu. "ya kwamba walitengeneza kwa mikono yao" au "ambayo walitengeneza wao wenyewe"

kile vidole vyao kimetengeneza ... nguzo za Ashera au sanamu za jua

Msemo wa pili unatambua vitu ambavyo watu walitengeneza. Kuzungumzia vidole hapa inasisitiza ya kuwa watu walizitengeneza, kwa hiyo vitu hivi sio miungu ya kweli. "nguzo za Ashera au sanamu za jua, ambayo walitengeneza wao wenyewe"

walitelekezwa kwa sababu ya watu wa Israeli

Inaweza kuwekwa wazi ni nani aliacha nchi hii. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ya kwamba Wahivi na Waamori waliacha baada ya watu wa Israeli kuja"

Isaiah 17:10

Kwa kuwa umesahau

Hapa "umesahau" ina maana ya watu wa Israeli. Neno "kusahau haimaanishi hawakuwa na kumbukumbu ya Mungu. Ina maana hawakumtii tena. "Kwa kuwa hamtii tena"

Mungu wa wokovu wako

"Mungu ambaye anakuokoa"

na umepuuzia mwamba wa nguvu yako

Hii inalinganisha Mungu na jiwe kubwa ambalo watu wanweza kupanda kutoka kwa adui zao au kujificha nyuma. "na wamemsahau Mungu, ambaye ni kama mwamba unaowalinda" au "na wamemsahau yule ambaye anawalinda"

mavuno yatashindwa

"hapatakuwa na matunda mengi kwa ajili yako kuvuna"

Isaiah 17:12

Vurumai ya watu wengi, kelele hiyo kama kelele za bahari

Vurumai ni sauti kubwa sana. "Sauti ya watu wengi, ambayo ni kubwa sana kama ya bahari"

kushuka kwa mataifa, kushuka huko kama kushuka kwa maji mengi

Majeshi ya maadui yanaonekana kuwa na nguvu sana ambayo hakuna awezaye kuwazuia. "mataifa wanakuja wakishuka kama maji mengi"

kushuka kwa mataifa

Neno "mataifa" lina maana ya majeshi ya mataifa hayo. "kushuka kwa majeshi ya maadui"

kama majani yaliyokufa juu ya milima kabla ya upepo ... kama majani yanavyozunguka kabla ya dhoruba

Misemo hii miwili ina maana moja. Majeshi wa maadui inaonekana kuwa na nguvu lakini Mungu atawazuia kwa urahisi na kuwafukuza mbali. "kama majani yaliyokufa juu ya milima ambayo upepo huipuliza mbali ... kama majani ambayo huzunguka na kupulizwa mbali ambapo dhoruba hukaribia"

hii ni sehemu ya wale

Kile kinachotokea kwao inazungumziwa kana kwamba ni sehemu ambayo wanarithi. "Hiki ndicho kinachotokea kwa wale"

wanaotupora ... wanaotuibia

Neno "..tupora ...tuibia" lina maana ya Isaya na watu wa Yuda.

Isaiah 18

Isaiah 18:1

Ole nchi yenye mchakarisho wa mabawa, ambayo ipo kando mwa mito ya Kushi

Maana za "mchakarisho wa mabawa" zawezekana kuwa 1) mabawa yanawakilisha mitumbwi ambayo ina matanga. "Ole wao ambao huishi katika nchi ng'ambo ya pili ya mito ya Kushi, ambao meli zao nyingi huonekana kama wadudu juu ya maji" au 2) mchakarisho wa mabawa una maana ya kelele ya wadudu wenye mabawa, huenda nzige.

katika bahari

Mto ulikuwa mpana sana, na watu wa Misri na Kushi waliutaja kama "bahari". "katika mto mkuu" au "katika Mto"

vyombo vya mafunjo

Mafunjo ni mmea mrefu ambao huota kando na Mto mkuu. Watu walifunga pamoja mafungu ya mafunjo kutengeneza makasia. "makasia ya mafunjo" au "makasia yanayotengenezwa kwa matete"

taifa refu na laini ... watu wanaogopwa mbali na karibu ... taifa lenye nguvu na kukanyaga chini, ambayo nchi yake mito huigawanya

Misemo hii yote inaelezea watu wa taifa moja.

taifa refu na laini

Neno "taifa" hapa lina maana ya watu wa taifa hilo. "taifa ambalo watu ni warefu na wana ngozi laini"

watu wanaogopwa mbali na karibu

Maneno "mbali" na "karibu" yanatumika pamoja kumaanisha "kila mahali". "watu ambao wanaogopwa kila mahali" au "watu ambao kila mtu duniani huwaogopa"

taifa lenye nguvu na kukanyaga chini

Kukanyaga chini inawakilisha kushinda mataifa mengine. "taifa ambalo lina nguvu na hushinda mataifa mengine"

mito huigawanya

Huenda hii ina maana ya mito mingi ambayo hutiririka katika taifa ili igawanye katika sehemu tofauti.

Isaiah 18:3

Kauli Kiunganishi

Mstari wa 3 unasema kile wajumbe katika 18:1 wanapaswa kusema kwa watu wa dunia.

Enyi wakazi wote wa duniani ... nyie mnaoishi juu ya dunia

Misemo hii miwili kimsingi ina maana moja. "Nyie watu wote wa duniani"

ishara itakapoinuliwa juu ya milima, tazama; na tarumbeta itakapopulizwa, sikiliza

Ishara na tarumbeta ilikuwa kuwaita watu vitani. Amri za kutazama na kusikiliza ni amri za kuzingatia kwa makini na kujiandaa kwa vita. "zingatia kwa makini pale ambapo ishara inainuliwa juu ya milima na tarumbeta inapopulizwa"

ishara itakapoinuliwa juu ya milima, tazama

Ishara ilikuwa bendera iliyotumika kuwaita watu vitani. Inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. Zingatia kwa makini pale utakapoona bendera ya vita juu ya milima".

tarumbeta itakapopulizwa, sikiliza

Tarumbeta zilitumika kuwaita watu vitani. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "zingatia kwa makini utakaposikia sauti ya tarumbeta za vita".

Isaiah 18:4

Taarifa ya Jumla

Mungu anatumia fumbo kuhusu mkulima katika shamba la mizabibu ili kufafanua kile atakachofanya kwa taifa fulani. Taifa hilo ni kati ya Kushi au adui wa Kushi.

Hiki ndicho Yahwe alichosema kwangu

"Yahwe aliniambia". Hapa neno "kwangu" ina maana ya Isaya.

Nitachunguza kwa utulivu kutoka kwenye nyuma yangu

Kile Mungu atakachochunguza kinaweza kuwekwa wazi. "Nitachunguza taifa hilo kwa utulivu kutoka nyumbani kwangu" au "Kutoka nyumbani kwangu, nitatazama kwa utulivu kile ambacho watu wa taifa hilo wanachofanya"

kama joto linalochemka pole pole katika mwanga wa jua, kama wingu la umande katika joto la mavuno

Misemo hii inaonyesha jinsi gani Mungu atazama taifa kwa utulivu.

Kabla ya mavuno

"Kabla ya mavuno ya zabibu"

pale ambapo uchanuzi umekamilika

Inaweza kuwekwa wazi ya kwamba hii ina maana ya kuchanuka juu ya mizabibu. "pale ambapo maua yamekamilisha kuota juu ya mizabibu"

atayakata matawi

Kama mkulima anaona ya kwamba tawi jipya halizai tunda, atalikata. "mkulima atakata matawi ambayo hayazai matunda"

makasi ya kupogolea

Mkasi wa kupogolea ni kisu ambacho watu hutumia kukata matawi katika mizabibu au mimea mingine.

atakata chini na kuondoa matawi yaliyotawanyika

Kama mkulima anaona ya kwamba tawi limeota sana na linafanya mzabibu wote kutozaa matunda mengi, ataukata na kuutupa.

Isaiah 18:6

Wataachwa pamoja

Inaonekana Mungu anabadilisha kutoka kuelezea fumbo na kuzungumzia moja kwa moja juu ya taifa. Hii inaweza kuwekwa wazi. "Wale ambao wanauawa wataachwa pamoja" au "Kama matawi yanayokatwa na kutupwa, miili ya wale ambao wameuawa wataachwa juu ya nchi"

Ndege watakuwa juu yao wakati wa kiangazi

"Ndege zitawala wakati wa kiangazi". Maneno "ndege" yana maana ya ndege ambao hula nyama ya miili iliyokufa.

wanyama wote wa duniani

"aina zote za wanyama pori"

watakuwa juu yao wakati wa baridi

"watawala katika kipindi cha baridi"

watu warefu na laini ... watu wanaogopwa mbali na karibu .... taifa lenye nguvu na kukanyaga chini, ambayo nchi yake imegawanywa na mito

Misemo hii yote inaelezea watu wa taifa kubwa.

watu warefu na laini

"watu ambao ni warefu na wenye ngozi laini"

watu wanaogopwa mbali na karibu

Maneno "mbali" na "karibu" yanatumika pamoja kumaanisha "kila mahali". "watu ambao wanaogopwa kila mahali" au "watu ambao kila mtu duniani anawaogopa".

taifa lenye nguvu na kukanyaga chini

Kukanyaga chini inawakilisha kushinda mataifa mengine. "taifa ambalo lina nguvu na hushinda mataifa mengine"

mpaka mahali penye jina la Yahwe wa majeshi, kwa mlima Sayuni

Neno "jina" lina maana ya Yahwe. "mpaka Mlima Sayuni, ambapo Yahwe wa majeshi hukaa"

Isaiah 19

Isaiah 19:1

Tazama

"Angalia" au "Sikiliza". Neno hili linaongeza msisitizo kwa kile kinachosemwa baadaye.

Yahwe anaendesha juu ya wingu jepesi

Yahwe anaonekana kupigwa picha hapa akiendesha juu ya wingu kana kwamba alikuwa akiendesha katika kibandawazi.

sanamu za Misri zinatetemeka mbele zake

Sanamu zinaelezwa kama kuwa na hisia za uoga Yahwe anapokaribia. "sanamu za Misri zinatetemeka kwa uoga mbele za Yahwe"

na mioyo ya Wamisri zinayeyuka ndani mwao

Moyo kuyeyuka kunawakilisha kupoteza ujasiri wake. "na Wamisri hawana ujasiri tena"

mwanamume dhidi ya jirani yake

Maneno "atapigana" inaeleweka kutoka kwa msemo uliopita. "mwanamume atapigana dhidi ya jirani yake"

mji utakuwa dhidi ya mji

Neno "mji" unawakilisha watu wa mji. "watu wa mji mmoja watapigana dhidi ya watu wa mji mwingine" au "watu kutoka miji tofauti watapigana dhidi yao wenyewe"

ufalme dhidi ya ufalme

Manebo "utakuwa" au "utapigana" inaeleweka kutoka kwa misemo ya nyuma. "ufalme utakuwa dhidi ya ufalme" au "ufalme utapigana dhidi ya ufalme"

ufalme dhidi ya ufalme

Neno "ufalme" una maana ya ufalme mdogo ndani ya Misri. Pia inaweza kuitwa mkoa. Inawakilisha watu wa ufalme huo au mkoa. "watu wa mkoa mwingine watakuwa dhidi ya watu wa mko mwingine" au "watu kutoka mikoa tofauti watapigana dhidi yao wenyewe"

Isaiah 19:3

Roho ya Misri itadhoofishwa kutoka kwa ndani. Nitaangamiza ushauri wake

Taifa la Misri linazungumziwa hapa kana kwamba lilikuwa mtu.

Roho ya Misri itadhoofishwa kutoka kwa ndani

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Nitadhoofisha roho ya Misri kwa ndani"

Nitaangamiza ushauri wake

Hii inaweza kuandikwa ili kwamba nomino dhahania "ushauri" inaelezwa kama kitenzi "shauri". "Nitawachangnaya wale amabo wanamshauri mfalme"

ingawa

"ingawa" hata kama"

waganga ... wachawi

Hawa ni watu ambao wanadai kuzungumza na wale ambao wamekufa.

Nitawapa Wamisri katika mikono ya bwana mkali

Hapa "mkono" ina maana ya nguvu na tawala. "Nitatoa Wamisri katika utawala wa bwana mkali"

hili ni tamko la Bwana , Yahwe wa majeshi

Nomino dhahania "tamko" linaweza kutafsiriwa kama kitenzi. "hivi ndivyo Bwana, Yahwe wa majeshi, anavyosema"

Isaiah 19:5

Maji ya bahari yatakauka, na mto utakauka na kuwa tupu

Wamisri walimaanisha Mto Nile kama "bahari". Misemo hii miwiwli ina maana. "Mto Nile utakauka kabisa"

itakuwa chafu

"kutoa harufu mbaya" au "kunuka"

itafifia

"kuwa chini"

matete na mianzi itasinyaa

"Matete" na "mianzi" ina maana ya aina mbili ya mimea ya maji. "mimea katika mto itakufa na kuoza"

Isaiah 19:7

mashamba yaliyopandwa ya Nile

"mashamba karibu na Mto Nile ambapo watu wamepanda mazao"

wavuvi watalia na kuomboleza, na wote ambao hurusha ndoano katika Mto wataomboleza, na wale ambao hutawanya nyavu katika maji watahuzunika

Misemo hii mitatu ina maana moja. Ikibidi, sababu ya wao kuhuzunika inaweza kuwekwa wazi. "Wavuvi ambao hushika samaki kwa ndoano au nyavu watabeba kwa kufa moyo kwa sababu samaki wa Nile watakuwa wamekufa"

hurusha ndoano katika Mto Nile

Ili kukamta smaki, baadhi ya watu waliweka chakula kidogo katika ndoano, kufunga ndoano katika kamba, na kurusha ndoano katika maji. Samaki anapojaribu kula chakula, mdomo wake unanaswa katika ndoano, na mtu huvuta samaki nje ya maji.

hurusha

"rusha"

kutawanya nyavu juu ya maji

Ili kukamata samaki, baadhi ya watu hutupa wavu juu ya maji. Samaki anapokamtwa ndani yake, wanavuta wavu na samaki nje ya maji.

Isaiah 19:9

Watumishi katika kitani kilichochanwa na wale ambao hufuma nguo nyeupe watakwajuka. Watumishi wa nguo wa Misri watapondwa

Misemo hii miwili ina maana moja. Ikibidi, sababu ya wao kufadhaika inaweza kuwekwa wazi. "Watengeneza kitani wa Misri wataaibishwa kwa sababu hakuna kitani"

Watumishi katika kitani kilichochanwa

"Wale ambao wanafanya kazi na kitani iliyochanwa"

kitani kilichochanwa

Kitani ni mmea ambao huota katika Mto Nile. Watu kuchana utembo wake ili kuzigawanyisha, na kuzitumia kutengeneza uzi kwa ajili ya nguo ya kitani.

watakwajuka

"wataaibika"

Watumishi wa nguo

"Watu wa Misri ambao hutengeneza nguo"

watapondwa

Kupondwa inawakilisha hali ya kukata tamaa. "atavunjika moyo"

wanaofanya kazi ya kuajiriwa

"wanaofanya kazi kwa malipo"

watahuzunika ndani mwao

"watajisikia huzuni sana"

Isaiah 19:11

Wakuu wa Soani ni wapumbavu kabisa. Ushauri wa washauri wenye hekima kabisa wa Farao umekuwa hauna maana

Misemo hii miwili ina maana moja. Aidha wakuu wa Soani ndio washauri wenye hekima kabisa au Farao, au kuna kundi lingine la watu ambalo pia linaonyeshwa kuwa pumbavu.

Soani

Huu ni mji katika Misri ya kaskazini.

Unawezaje kusema kwa Farao ... wafalme?

Isaya anatumia swali kukejeli wale walio Misri wanaodai kuwa na hekima. "Mnasema kwa upumbavu kwa Farao ... wafalme"

Wako wapi basi wanaume wenu wenye hekima?

Isaya anatumia swali kukejeli wanaume wenye hekima. Neno "wenu" ina maana ya Farao. "Hauna wanaume wowote wenye hekima" au "Wanaume wako wenye hekima ni wapumbavu"

Waache wakuambie na kufanya kujulikana kile Yahwe wa majeshi anapanga kuhusu Misri.

isaya anadokeza ya kwamba wanamume wenye hekima wanatakiwa kuweza kuelewa mipango ya Mungu, lakini Isaya haamini kiukweli kuwa wana hekima. "kama walikuwa na hekima kweli, wangeweza kukuambia kile Yahwe wa majeshi anavyopanga kuhusu Misri"

Isaiah 19:13

wamefanya Misri ipotoke, ambayo ni jiwe la pembeni la makabila yake

Wakuu wa Soani na Nofu wanazungumziwa kana kwamba wao ni jiwe la pembeni la majengo kwa sababu wao ni sehemu muhimu katika jamii. "viongozi wamefanya Misri kupotoka"

wakuu wa Soani

Soani ni mji kaskazini mwa Misri.

Nofu

Huu ni mji katika sehemu ya kaskazini ya Misri.

wamefanya Misri ipotoke

Neno "Misri" linawakilisha watu wa Misri. Kupotoka kunawakilisha kufanya kilicho kibaya. "kufanya watu wa Misri kupotoka" au "kufanya watu wa Misri kufanya kilicho kibaya"

Yahwe amechanganya roho ya upotoshaji miongoni mwake

Isaya anazungumzia hukumu ya Yahwe kana kwamba Misri ilikuwa kikapu cha divai. Anazungumzia Yahwe kusababisha mawazo ya viongozi kupotoshwa kana kwamba mawazo yao yaliyopotoka yalikuwa kimiminiko ambacho Yahwe alichanganya kwa divai. "Yahwe amewahukumu kwa mawazo yao yaliyopotoka" au "Yahwe amewahukumu Misri kwa kupotosha mawazo ya viongozi wao, kama vinywaji vinavyolewesha huchanganya mawazo ya watu"

upotoshaji

"upotovu" au "mchafuko"

miongoni mwake

Hapa "mwake" ina maana ya Misri. Mataifa mara kwa mara huzungumziwa kana kwmaba ilikuwa wanawake. "ndani ya Misri"

wameiongoza Misri kupotea

Hapa "wameiongoza" ina maana ya viongozi wanaoelezwa katika mistari iliyopita. Neno "Misri" inawakilisha watu wa Misri. "wakuu wamewaongoza watu wa Misri kupotoka"

wameiongoza Misri kupotea

Kuongoza watu kupotoka inawakilisha kuwashawi kufanya kilicho kibaya.

kama mlevi anayepepesuka katika matapishi yake

Isaya anazungumzia watu wa Misri kufanya kilicho kibaya kana kwamba walifanywa kuzurura kama mtu mlevi.

kama kichwa au mkia

"Kichwa" ni sehemu ya mnyama au mtu anayopenda awe, inawakilisha kiongozi. "Mkia" ni kinyume na inawakilisha watu wanaofuata. "kama kiongozi au mfuasi"

tawi la mnazi au tete

"tawi la mnazi" huota juu ya mti na linawakilisha watu ambao ni tajiri na muhimu. "Tete" huota katika maji mafupi na inawakilisha watu ambao ni maskini na wasio na umuhimu. "kama wao ni muhimu au sio muhimu" au "kama ni tajiri au maskini"

Isaiah 19:16

Wamisri watakuwa kama wanawake

Hii inasisitiza ya kwamba watu wa Misri wataogopa na kutojiweza Mungu anapowaadhibu.

kwa sababu ya mkono wa Yahwe wa majeshi usiosifiwa

Hapa "mkono" una maana ya nguvu ya Mungu, na kuinua mkono dhidi yao inawakilisha kuwaadhibu wao. "kwa sababu Yahwe wa majeshi ameinua mkono wake wa nguvu kuwaadhibu"

nchi ya Yuda itakuwa sababu ya kupepesuka kwa Misri

"nchi ya Yuda" na "Misri" ina maana ya watu katika maeneo hayo. Wamisri watapepesuka kwa sababu wanaogopa. "Watu wa Yuda watasababisha Wamisri kupepesuka" au "Watu wa Yuda watasababisha Wamisri kuogopa sana"

Wakati wowote mtu yeyote anawakumbusha juu yake, wataogopa

Hapa, "anawakumbusha" na "wataogopa" ina maana ya Wamisri na "yake" ina maana ya watu wa Yuda. "Wakati wowote mtu yeyote anawakumbusha Wamisri wa watu wa Yuda, Wamisri wataogopa"

Isaiah 19:18

kutakuwa na miji mitano katika nchi ya Misri ambayo inazungumza

Hii ina maana ya watu wa miji ile. "watu katika miji mitano ya Misri watazungumza"

lugha ya Kaanani

Hii ina maana ya Kiebrania, lugha ya watu wa Mungu wanaoishi katika nchi ya Kanaani. "lugha ya watu wa Kanaani"

kutoa kiapo cha utii

"ahidi kuwa mwaminifu"

Moja ya miji hii itaitwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Watu wataziita moja ya miji hii"

itaitwa Mji wa Jua

Haipo wazi kama neno la Kiebrania linalotafsiriwa "Jua" hapa lina maana ya "jua" au "uharibifu". Haipo wazi ni nini jina linasema juu ya mji. "mji unoitwa 'Mji wa Jua'" au "mji unaoitwa "Mji wa Uharibifu"

Isaiah 19:19

jiwe la nguzo katika mpaka wa Yahwe

Msemo "mpaka" ina maana ya mpaka wa Misri. "jiwe la nguzo kwa Yahwe katika mpaka wa Misri"

itakuwa kama ishara na shahidi kwa Yahwe wa majeshi katika nchi ya Misri

Nomino dhahania "ishara" na "shahidi" inaweza kuelezwa kwa vitenzi "onyesha" na kuthibitisha. "Dhabahu itaonyesha na kuthibitisha ya kwamba Yahwe wa majeshi yupo katika nchi ya Misri"

kwa Yahwe wa majeshi katika nchi ya Misri

Yahwe kuwa katika nchi ya Misri inawakilsiha watu wa Misri kumuabudu yeye. "ya kwamba watu katika nchi ya Misri humwabudu Yahwe wa majeshi"

Watakapomlilia

"Wamisri watakapolia"

kwa sababu ya wakandamizaji

"kwa sababu watu wanatendea kwa ukatili" au "kwa sababu wengine wanasababisha wao wateseke"

atawatumia mkombozi na mtetezi

"Yahwe atamtuma mtu kuwaokoa na kuwatetea Wamisri"

atawaokoa

Nani ambaye Yahwe atatetea kwao inaweza kuwekwa wazi. "Yahwe atawaokoa Wamisri kutoka kwa wakandamizaji wao"

Isaiah 19:21

Yahwe atajulikana kwa Misri

Hapa "Misri" ina maana ya watu wa Misri. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe atawafanya watu wa Misri kumjua"

watamtambua Yahwe

"watapokea ukweli juu ya Yahwe" au "watakubaliana na ukweli juu ya Yahwe"

Watamwabudu

Kitu cha ibaada yao kinaweza kuwekwa wazi. "Watamwabudu Yahwe"

watatoa viapo kwa Yahwe na kuzitimiza

'"watatoa ahadi kwa Yahwe na kuzishika" au "'watatoa ahadi kwa Yahwe na watafanya kile walichokiahidi kufanya"

Yahwe ataiumiza Misri

Hapa, "Misri" ina maana ya watu wa Misri. "Yahwe ataumiza watu wa Misri"

umiza

"kupiga" au "kuadhibu"

kuwaumiza na kuwaponya

Neno "wao" linaeleweka katika msemo huu. "kuwaumiza wao na kuwaponya wao"

kuwaumiza na kuwaponya

Jinsi msemo huu unavyohusiana na msemo kabla yake unaweza kuwekwa wazi kwa maneno '"baada" na "pia". "na baada yake kuwaumiiza, pia atawaponya"

Isaiah 19:23

kutakuwa na barabara

Barabara ni njia kubwa ambayo watu wanaweza kusafiri

Muashuru atakuja

"Muashuru" ina maana ya mtu kutoka Ashuru lakini inawakilisha yeyote kutoka Ashuru ambaye anatoka Misri. "Waashuru atakuja"

na Mmisri mpaka Ashuru

Neno "atakuja" linaeleweka. "na Mmisri atakuja mpaka Ashuru"

Mmisri

Hii ina maana ya mtu kutoka Misri, lakini inawakilisha yeyote kutoka Misri ambaye anakuja Ashuru. "Wamisri"

Mmisri ataabudu pamoja na Waashuru

Kitu cha ibaada yao kinaweza kuwekwa wazi. . "Wamisri na Waashuru watamwabudu Yahwe"

Isaiah 19:24

Israeli atakuwa wa tatu pamoja na Misri na Ashuru

Majina ya mataifa matatu yanawakiliisha watu wa mataifa hayo. "Waisraeli watakuwa wa tatu pamoja na Wamisri na Waashuru"

atakuwa wa tatu pamoja na

Maana zaweza kuwa 1) "kujiunga pamoja na" au 2) "kuwa na baraka ya tatu pamoja na" au 3) "'kuwa sawa na"

Misri na ibarikiwe, watu wangu; Ashuru, kazi ya mikono yangu; na Israeli, urithi wangu

Majina ya mataifa matatu yana maana ya watu wa mataifa yale. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Nimekubariki, watu wa Misri, kwa sababu wewe ni mtu wangu; na nimekubariki, watu wa Ashuru, kwa sababu nimekuumba; na nimekubariki, watu wa Israeli, kwa sababu ninakumiliki kwa usalama"

kazi ya mikono yangu

Hapa "mikono" ina maana ya nguvu ya Mungu na matendo.

Isaiah 20

Isaiah 20:1

jemadari yule

Jina la kamanda mkuu wa majeshi ya Ashuru

Sargoni

jina la mfalme wa Ashuru

alipigana dhidi ya Ashdodi na kuuchukua

Ashdodi ina maana ya jeshi la Ashdodi. "alipigana dhidi ya jeshi la Ashdodi na kulishinda"

kutembea uchi na peku

"kutembea tembea bila nguo na bila ndara". Hapa neno "uchi" huenda ina maana ya kuvaa nguo zake za ndani pekee.

Isaiah 20:3

na ishara

"na tahadhari"

kuhusu Misri na kuhusu Kushi

Majina ya sehemu yana maana ya watu wake. "kuhusu watu wa Misri na watu wa Kushi"

mfalme wa Ashuru atawaongoza mbali mateka

Mfalme huamrisha jeshi lake kufanya kazi hii. "mfalme wa Ashuru atalifanya jeshi lake kuwaongoza mbali mateka"

atawaongoza mbali mateka wa Misri, na walio hamishwa wa Kushi

Inaweza kuwekwa wazi ya kwamba watashambulia kwanza na kukamata watu. "watashambulia Misri na Kushi na kukamata watu wake na kuwaongoza mbali"

kwa aibu ya Misri

Misri ina maana ya watu wa Misri. "ambayo italeta aibu juu ya watu wa Misri"

Isaiah 20:5

watafadhaishwa na kuaibika

"kuogopa na kupata aibu"

kwa sababu ya Kushi tumaini lao na ya Misri utukufu wao

Tumaini na utukufu ina maana ya imani yao katika nguvu ya jeshi ya nchi hizi. "kwa sababu waliamini katika nguvu ya majeshi ya Kushi na Misri"

wakazi wa pwani hizi

watu ambao waliishi katika nchi zinazopakana na Bahari ya Mediteranea

ambapo tulikimbilia kwa ajili ya msaada kukombolewa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "ambapo tuliporokea ili kwamba waweze kutukomboa"

na sasa, tutatorokaje?

Mwandishi anatumia swali hili kusisitiza jinsi hali yao ilivyokosa tumaini. "Sasa hakuna njia kwa ajili yetu kutoroka!"

Isaiah 21

Isaiah 21:1

Tamko

"Hivi ndivyo Yahwe anavyotamka" au "Huu ni ujumbe wa Yahwe"

kuhusu jangwa karibu na bahari

Hii ina maana ya watu ambao wanaishi babeli kama kuwa jangwa, ingawa Mungu bado hajapafanya kuwa jangwa. Tukio hili hakikalitatokea. "kuhusu watu wanaoishi katikanchi ambayo punde itakuwa jangwa"

Kama upepo wa dhoruba unavyofyeka katikati ya Negebu

Isaya analinganihsa jeshi ambalo litashambulia watu na dhoruba yenye upepo mkali. Watakuwa na kasi na nguvu.

kutoka nyikani

Hapa "nyikani" ina maana ya nyika ya Yuda.

kutoka katika nchi ya kutisha

Jeshi linatokana na watu ambao husababisha hofu kubwa.

maono ya kudhihikisha yameletwa kwangu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Yahwe alinionyesha maono ya kusumbua akili"

mwanamume mdanganyifu anafanya udanganyifu

"wale wanaodanganya watadanganya"

na mharibifu huharibu

"na wale wanaoharibu wataharibu"

Nenda juu na ushambulie, Elamu; izingire, Umedi

Katika maono yaliyopatiwa Isaya, Yahwe anazungumza kwa majeshi ya Elamu na Umedi kana kwamba walikuwa wakimsikiliza.

Nenda juu na ushambulie, Elamu; izingire, Umedi

Inaeleweka ya kwamba wanapaswa kushambulia Wababeli. "Nenda juu na ushambulie Wababeli, nyie wanajeshi wa Elamu; nendeni na muwazingire Wababeli, nyie wanajeshi wa Umedi"

Elamu ... Umedi

Hapa "Elamu" na "Umedi" inawakilisha wanajeshi kutoka maeneo haya.

Nitakomesha minung'uniko yake yote

Hapa "yake" inawakilisha watu wote ambao wanateseka kwa sababu ya Wababeli. Yahwe atasababisha kuacha kulalamika atakapotuma majeshi ya elamu na Umedi kuangamiza Wababeli.

Isaiah 21:3

viuno vyangu vimejaa maumivu

Maono haya ambayo Isaya anayaona yanasumbua yanasababisha maumivu kwake. Hapa anaelezea maumivu na mkakamao katika sehemu ya kati ya mwili wake.

maumivu kama maumivu ya mwanamke katika uchungu vimenikamata

Isaya analinganisha maumivu yake na maumivu ya mwanamke anayezaa. Hii inasisitiza maumivu makubwa anayosikia.

nimeinama chini kwa kile nilichosikia

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Kile nilichosikia kimenisababisha kuinama chini kwa maumivu"

nimesumbuliwa kwa kile nilichokiona

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Kile nilichoona kimenisumbua sana"

Moyo wangu unadunda, ninatetemeka kwa hofu

"Moyo wangu unapiga haraka na ninatetemeka"

Isaiah 21:5

Wanaandaa

Hapa "wanaandaa" ina maana ya viongozi wa Babeli.

andaa meza

Hapa "meza" inawakilisha chakula ambacho watu watakula katika karamu.

inuka, wakuu

Hapa "wakuu" ina maana kwa ujumla wanamume wenye mamlaka na sio lazima wana wa wafalme.

pakeni ngao zenu kwa mafuta

Wanajeshi wangepaka mafuta juu ngao zao za ngozi ili kwamba ziweze kuwa laini na zisipasuke wakati wa vita.

Isaiah 21:6

weka mlinzi

"mwambie mlinzi asimame juu ya ukuta wa Yerusalemu"

kibandawazi, jozi ya wapanda farasi

"mwanajeshi anaendesha katika kibandawazi, jozi ya farasi ikiivuta"

Isaiah 21:8

Bwana, nasimama juu ya mnara

Hapa "Bwana" ina maana ya mtu mwenye mamlaka ambaye alimuamuru mlinzi kusimama juu ya ukuta wa Yerusalemu.

Babeli imeanguka, imeanguka

Babeli kushindwa kabisa na adui zake inazungumziwa kana kwamba Babeli imeanguka. Hapa "Babeli" ni mfano wa maneno unawakilisha watu wa Babeli. "Watu wa Babeli wameshindwa kabisa"

imeanguka, imeanguka

Neno "imeanguka" inarudiwa kusisitiza ya kwamba watu wa Babeli walishindwa kabisa na adui zao.

Isaiah 21:10

Wale niliowapukuta na kuwapembua, watoto wa sakafu yangu ya kupukuchua

Watu wa Israeli kuteseka kwa sababu ya Wababeli inazungumziwa kana kwamba watu walikuwa nafaka ambayo ilipukukutwa na kupembuliwa.

niliowapukuta

neno "yangu" ina maana ya Isaya.

Yahwe wa majeshi

Yahwe wa majeshi ya Israeli.

Isaiah 21:11

Tamko

"Hivi ndivyo Yahwe anavyotamka" au "Huu ni ujumbe kutoka kwa Yahwe"

kuhusu Duma

Hili ni jina lingine kwa ajili ya Edomu. Hapa "Duma" inawakilisha watu wanaoishi kule. "kuhusu watu wa Duma" au "kuhusu watu wa Edomu"

Mtu ananiita kwangu

Hapa "ananiita" ina maana ya Isaya.

Seiri

Hili ni jina la milima ya magharibi mwa Edomu.

Mlinzi, nini kimebaki usiku? Mlinzi, nini kimebaki usiku?

Hii inarudiwa kusisitiza ya kwamba mtu yule anayeuliza swali ana wasiwasi na woga.

kama unataka kuuliza, basi uliza; na urudi tena

"Niulize sasa kile unachotaka kujua, lakini pia uje baadaye uniulize tena"

Isaiah 21:13

Tamko

"Hivi ndivyo Yahwe anavyotamka" au "Huu ni ujumbe kutoka kwa Yahwe"

kuhusu Arabuni

Arabuni ina maana ya idadi ya watu wa Arabuni. "kuhusu watu wa Arabuni"

Katika nyika ya Arabuni

Arabuni haina msitu. "mbali kutoka na barabara ya Arabuni" au "Nje katika vichaka vya Arabuni"

misafara

kikundi cha watu wanaosafiri pamoja

Wadedani

Hili ni kundi la watu ambao wanaishi Arabuni.

nchi ya Tema

Hili ni jina la mji Arabuni.

wakimbizi

Mkimbizi ni mtu ambaye hukimbia mbali ili adui wake asimkamate.

kwa mkate

Hapa "mkate" inawakilisha chakula kwa ujumla.

kutoka kwa upanga, kutoka kwa upanga uliotolewa, kutoka kwa upinde uliopindwa

Hapa "upanga" na "upinde" unawakilisha wanajeshi wanaoshambulia wakazi wa Tema. "kutoka kwa adui zao ambao huwashambulia kwa upanga na upinde"

kutoka kwa uzito wa vita

Hofu kuu na mateso ambayo inapitiwa wakati wa vita inazungumziwa kana kwamba vita ilikuwa uzito mkubwa juu ya watu. "kutoka na vitisho vya vita"

Isaiah 21:16

kama mwajiriwa alivyoajiriwa kwa mwaka atakavyoona

"kama mwajiri aliyeajiriwa atakavyohesabu siku za mwaka". Mtumishi aliyeajiriwa ni mwangalifu kuhesabu siku ili kwamba afanye kazi kwa muda husika anaolipwa kufanya. Hii ina maana Kedari itashindwa ndani ya mwaka mmoja kamili.

wa Kedari

Hili ni eneo kule Uarabuni. Kedari inawakilisha idadi ya watu wa Kedari. "ya watu wa Kedari"

Isaiah 22

Isaiah 22:1

Tamko

"Hivi ndivyo Yahwe anachotamka" au "Huu ni ujumbe wa Yahwe"

juu ya bondo la maono

Hapa "Bonde" ina maana ya wale ambao wanaishi katika bonde, yaani, Yerusalemu. "juu ya wale ambao wanaishi katika Bonde la Maono" au "kuhusu wale ambao wanaishi Yerusalemu"

Ni sababu ipi ambayo wote mmekwenda juu ya dari za nyumba

Isaya anatumia swali kukaripia watu wa Yua. "'Hautakiwi kwend na kusimama juu ya dari za nyumba"

mji uliojaa shangwe

"mji uliojaa watu wanaoshangilia"

Wafu wako hawakuawa kwa upanga

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Wanajeshi maadui hawakuwaua watu wako"

kwa upanga

Hapa "upanga" inawakilisha wanajeshi ambao hupigana vitani.

Isaiah 22:3

lakini walikamatwa bila upinde

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "lakini adui aliwakamata watawala wako ambao hata hawakuwa wakibeba upinde"

wote walikamatwa na kushikwa pamoja

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "adui aliwakamata na kuwashika wote pamoja"

Kwa hiyo nikasema

Hapa "Mimi" ina maana ya Isaya

wa binti wa watu wangu

Hapa "binti" inawakilisha watu na inaweza kudokeza hisia za Isaya za upendo kwa ajili yao. "'wa watu wangu ambao nampenda" au "wa watu wangu"

Isaiah 22:5

Kwa maana kuna siku

Hapa "siku" ina maana ya kipindii kirefu cha muda. "Kwa maana kutakuwa na muda"

ya ghasia, kukanyagwa chini, na kuchanganyikiwa kwa ajili ya Bwana, Yahwe wa majeshi

"pale Yahwe wa majeshi atasababisha hofu kubwa, kukanyagwa chini, na kuchanganyikiwa

kukanyagwa chini

Maana zaweza kuwa 1) hii ina maana ya wanajeshi wakitembea au 2) watu kwa ujumla wanakimbia kwa hofu kubwa na kutokuwa na uhakika wapi pa kwenda.

katika Bonde la Maono

Hapa "Bonde" ina maana ya wale ambao wanaishi katika bonde, yaani, Yerusalemu. "juu ya wale ambao wanaishi katika Bonde la Maono" au "kuhusu wale ambao wanaishi Yerusalemu"

watu kulia katika milima

Maana zaweza kuwa 1) "watu katika milima watasikia sauti zao" au 2) "milio ya watu inasikika katika milima"

Elamu anabeba podo

Podo ni mfuko wa kubeba mishale na inawakilisha silaha za mpiga mshale. "Wanajeshi wa Elamu huchukua upinde zao na mishale"

Kiri anaweka wazi ngao

Hapa "Kiri" inawakilisha wanajeshi. "wanajeshi wa Kiri watabeba ngao zao nje ya makasha yao"

Kiri

Kiri ni mji wa Media.

mabonde yako mazuri

Hapa "yako" ina maana ya watu wa Yerusalemu. Isaya hajijumlishi mwenyewe kama mmoja wa watu wa Yerusalemu. "mabonde yetu mazuri"

Isaiah 22:8

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kufafanua kipindi katika siku za usoni ambapo jeshi litashambulia watu wa Yerusalemu. Vitenzi vya wakati uliopita vinaweza kutafsiriwa kwa vitenzi vya wakati unaokuja.

Aliondoa ulinzi wa Yuda

Nomino dhahania "ulinzi" inaweza kuwekwa kama kitenzi. "Yahwe atachukua kila kitu ambacho kiliwalinda watu wa Yuda"

ukaangalia katika siku hiyo kwa ajili ya silaha

Hapa msemo "kuangalia" ina maana ya kuamini katika jambo. "ili kujilinda utachukua silaha"

Kasri ya Msitu

Hii ilikuwa sehemu ya hekalu Yerusalemu ambapo walihifadhi silaha zao.

ulikusanya maji ya dimbwi la chini

Watu watahifadhi maji ili kwamba waweze kuwa na maji ya kunywa ya kutosha huku adui zao wakizunguka mji.

Isaiah 22:10

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kufafanua kipindi katika siku za usoni ambapo jeshi litashambulia watu wa Yerusalemu.

Ulihesabu nyumba

Hapa "hesabu" ina maana ya walikagua nyumba kutafuta nyezno kuwasaidia kujenga tena ukuta wa mji.

Ulitengeneza bwawa

"Ulitengeza sehemu ya kuhifadhi"

katikati ya kuta mbili

Haipo wazi Isaya alikuwa akimaanisha nini kwa kuta mbili. Cha msingi ni kwamba walijenga bwawa katikati ya kuta za mji.

anayetengeza mji

Hii ina maana ya Yahwe.

Isaiah 22:12

Yahwe wa majeshi

Yahwe wa majeshi ya Israeli.

kwa vichwa vilivyonyoa

Hii ilikwa ishara ya maombolezo na kutubu.

na tule na kunywa, kwa maana kesho tutakufa

Hapa "kula na kunywa" inawakilisha kuwa na sherehe na kuendekeza kula chakula na divai. "bora tupate starehe sasa kwa kula na kunywa vyote tunavyotaka, kwa maana tutakufa hivi punde"

Hii ilifunuliiwa masikioni mwangu na Yahwe wa majeshi

Hapa "masikio" inawakilisha Isaya kama kamili. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe wa majeshi alifunua hili kwangu"

Hakika udhalimu huu hautasamehewa, hata utakapokufa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Hakika sitakusamehe kwa ajili ya vitu hivi vya dhambi ulivyofanya, hata utakapokufa"

hata utakapokufa

Maana zaweza kuwa 1) Yahwe hatawasamehe, hata baada yao kufa au 2) Yahwe hatawasamehe mpaka wafe.

Isaiah 22:15

Shebna

Hili ni jina la msimamizi wa kasri ya mfalme huko Yerusalemu.

ambaye yupo juu ya nyumba

Hapa "nyumba" inawakilisha wale walio katika kasri ya mfalme. "ni nani aliye msimamizi wa wale ambao wanafanya kazi katika kasri"

Unafanya nini hapa na nani amekupa ruhusa ... katika mwamba?

Yahwe anatumia swalii hili kumkaripia Shebna. "Hauna haki ... katika mwamba!"

kukata kaburi ... kuchonga kaburi ... kuchonga sehemu ya kupumzika

Misemo hii mitatu yote ina maana ya kutengeneza kaburi la kuzika.

juu ya marefu

Watu muhimu zaidi wa Israel walikuwa na makaburi katika sehemu za juu.

Isaiah 22:17

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza ujumbe wa Mungu kwa Shebna.

Hakika atakuzungushazungusha, na kukurusha kama mpira kwa nchi kubwa mno

Wanajeshi maadui kuja na kumchukua Shebna kama mateka kwa nchi ya kigeni inazungumziwa kana kwamba Yahwe alikuwa akimrusha kama mpira katika nch nyingine.

utakuwa aibu ya nyumba ya bwana wako

Hapa "nyumba" inawakilisha watu ambao wanafanya kazi katiika kasri ya mfalme. "utasababisha aibu kwa wale wote walio ndani ya kasri ya bwana wako"

Nitakusukuma kutoka katika ofisi yako na kutoka katika kituo chako. Utavutwa chini

Yahwe kusababisha Shebna kutofanya kazi tena katika kasri ya mfalme inazungumzwa kana kwamba Yahwe atamtupa katika ardhi.

Utavutwa chini

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Nitakuleta chini kutoka katika nafasi yako ya juu"

Isaiah 22:20

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza ujumbe wa Mungu kwa Shebna.

Itakuja kuwa katika siku hiyo

Hapa "siku" inawakilisha kipindi kwa ujumla. "'Itatokea katika kipindi hicho"

Eliakimu ... Hilkia

Haya ni majina ya wanamume.

Nitamvisha kwa gwanda lako na kumwekea juu yake mshipi wako

Yahwe kusababisha Eliakimu kuchukua nafasi ya Shebna katika kasri ya mfalme inazungumziwa kana kwamba Yahwe atamvisha Eliakimu katika nguo za Shebna ambazo zinawakilisha mamlaka yake katika kasri ya mfalme.

gwanda lako ... mshipi wako

Hapa gwanda na mshipi inawakilisha mamlaka katika kasri ya mfalme.

mshipi

Hii ni kipande cha nguo ambacho watu huvaa kuzunguka kiuno au kupita kifuani.

katika mkono wake

Hapa "mkono" unawakilisha nguvu na utawala. "kwake"

Atakuwa baba

Eliakimu kutunza na kulinda watu wa Yuda inazungumziwa kana kwamba angekuwa baba yao. "Atakuwa kama baba"

katika nyumba ya Yuda

Hapa "nyumba" inawakilisha watu. "kwa watu wa Yuda"

Nitaweka ufunguo wa nyumba ya Daudi juu ya bega lake ... hakuna atakayefungua

Hapa "ufunguo" inawakilisha mamlaka. Hii inazungumzia Eliakimu kuwa na mamlaka ambayo hakuna mtu awezaye kumzuia kana kwamba alikuwa na ufunguo wa kasri na hakuna mtu mwingine awezaye kufunga au kufungua mlango. "Nitamweka kuwa msimamizi wa wale ambao hufanya kazi katika kasri ya mfalme, na anapofanya maamuzi hakuna atakayeweza kumpinga"

Isaiah 22:23

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kufafanua Eliakimu, ambaye atachukua nafasi ya Shebna katika kasri ya mfalme.

Nitamkaza, kigingi katika sehemu salama

Yahwe kusababisha mamlaka ya Eliakimu kuwa na nguvu na salama katika kasri ya mfalme inazungumziwa kana kwamba Eliakimu alikuwa kigingi na Yahwe atamweka kwa uthabiti katika kuta wa kasri.

atakuja kuwa kiti cha utukufu kwa ajili ya nyumba ya baba yake

Hapa "kiti cha utukufu" inawakilisha sehemu ya heshima. "Eliakimu ataleta heshima kwa familia yake"

nyumba ya baba yake

Hapa "nyumba" inawakilisha familia. "familia ya baba yake" au "familia yake"

Watamng'ang'ania yeye utukufu wote wa nyumba ya baba yake

Yahwe kusababisha familia nzima ya Eliakimu kuheshimiwa kwa sababu ya Eliakimu inazungumziwa kana kwamba Eliakimu alikuwa kigingi katika ukuta na familia yake ilikuwa kitu ambacho kinaning'inia juu ya kigingi. "Watatoa heshima kwa familia yake yote kwa sababu yake"

kila chombo kidogo kutoka katika vikombe kwa majagi yote

Hii inaendeleza kuzungumza juu ya Eliakimu kama kigingi. Mtoto wake atakuwa kama vikombe ambavyo vitaning'inia juu ya kigingi. Hii ina maana vizazi vyake vitaheshimika kwa sababu yake.

vikombe kwa majagi yote

Kikombe ni chombo kidogo ambacho kinashikilia maji. Jagi ni chombo kikubwa ambacho kinashikilia maji.

Isaiah 22:25

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza picha kutoka katika mistari ya nyuma.

Katika siku hiyo

Hapa "siku" inawakilisha kipindi kwa ujumla. "Katika kipindi hicho"

tamko la Yahwe wa majeshi

Hii inaweza kuandikwa ili kwamba nomino dhahania "tamko" ielezwe kama kitenzi "tamka" au "sema kwa dhati". "hivi ndivyo Yahwe wa majeshi alivyotamka" au "hivi ndivyo kile Yahwe wa majeshi alivyosema kwa dhati"

kigingi kuzamishwa katika sehemu imara ... utakatwa

Yahwe kusababisha Shebna kupoteza mamlaka yake katika kasri ya mfalme inazungumziwa kana kwamba Shebna ilikuwa kigingi katika ukuta ambacho hupasuka na kuanguka ardhini. Hii inasisitiza ya kwamba Shebna alifikiri mamlaka yake yalikuwa salama lakini Mungu atamwondoa.

uzito ambao ulikuwa juu yake utakatwa

Hapa "uzito" inawakilisha nguvu ya Shebna na mamlaka. Inazungumzia kana kwamba ilikuwa kitu kinachoning'inia juu ya kigingi ambacho kinachowakilisha Shebna. Yahwe kusababisha Shebna kupoteza nguvu yake na mamlaka inazungumziwa kana kwamba mtu alikuwa akikata kitu ambacho kilikuwa kinaning'inia juu ya kigingi.

Isaiah 23

Isaiah 23:1

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kusema kile ambacho Mungu amehukumu dhidi ya mataifa katika 13:1-23:18

Tamko kuhusu Tiro

"Hivi ndivyo Yahwe anavyotamka kuhusu Tiro"

Lia kwa sauti kali, enyi meli za Tarshishi

Hapa "meli" inawakilisha wanamume katika meli hizo. Isaya anazungumza na wanamume katika meli za Tarshishi kana kwamba zinaweza kumsikia. "Paza sauti kwa kukata tamaa enyi wanamume katika meli za Tarshishi"

bandari

eneo la bahari ambalo lipo karibu na nchi na salama kwa ajili ya meli

kutoka katika nchi ya Kupro imefunuliwa kwao

Msemo huu unaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "wanamume walisikia kuhusu Tiro walipokuwa katika nchi ya Kupro"

Kaeni kimya, nyie wakazi wa pwani

Isaya anazungumza na watu wanaoishi katika pwani kana kwamba wanaweza kumsikia.

Kaeni kimya

Hii ni lahaja. Hapa ukimya una maana ya kuashiria mshtuko na mshangao. "Ushtuke"

katika pwani

"pwani" ni nchi ambayo ipo karibu an inazunguka bahari. Hapa ina maana ya watu wanaoishi Wafinisia wanaopakana na bahari ya Mediteranea.

mfanya biashara wa Sidoni, ambaye anasafiri juu ya bahari, amekujaza

Hapa "mfanya biashara" ina maana ya "wafanya biashara wengi". "wafanya biashara wa Sidoni, ambao wanasafiri juu ya bahari, wamekufanya uwe tajiri"

Juu ya maji makuu kulikuwa na nafaka ya Shihori

Shihori ilikuwa jina la bonde karibu na Mto wa Nile katika Misri lijulikanalo kwa uzalishaji wake wa nafaka. "Wanamume walisafiri juu ya bahari kuu kusafirisha nafaka kutoka Shihori ndani ya Misri"

mavuno ya Nile yalikuwa mazao yake

Nafaka ilivunwa karibu na Mto na kusafirishwa katika mto na kisha mpaka Wafinisia.

mazao yake

"mazao yake". Ilikuwa kawaida kumaanisha mto kama "yake"

ikaja kuwa kitivo cha biashara cha mataifa

Kitivo cha biashara ni tendo la kununua na kuuza bidhaa. Hapa "mataifa" inawakilisha watu. "ulikuwa pale ambapo watu kutoka mataifa mengine walikuja kununua na kuuza bidhaa"

Isaiah 23:4

kwa maana bahari imeongea, mwenye uwezo wa bahari ... wala kukuza wanawake wachanga

Maana zaweza kuwa 1) Yahwe anaelezea mji wa Tiro kama mama ambaye huzungumza kuhusu watu wanaoishi katika mji kama watoto wake, au 2) Yahwe anafafanua Bahari ya Mediteranea kama ikizungumza. Watu wa Tiro walichukulia bahari mungu wao na baba. Katika maana mojawapo msemaji anaomboleza kwa sababu watoto wake wameangamizwa.

Isaiah 23:6

Vuka mpaka Tarshishi

"Tengeneza njia yako mpaka Tarshishi". Tarshishi ilikuwa nchi ya mbali watu wa Tiro walisafiri kufanya biashara. Itakuwa sehemu pekee ya usalama kwa wale wanaotoroka kutoka Tiro.

Je! hiki kimetokea kwako, mji wenye furaha, ambao asili yake inatoka kipindi cha zamani ... kukaa?

Yahwe anatumia swali kukejeli Tiro. Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Hili hasa limetokea kwako ambaye ulikuwa umejaa furaha katika mji wa zamani wa tiro .. kukaa."

mji wenye furaha

Hapa "mji" unawakilisha watu. "watu wenye furaha ambao waliishi katika mji wa Tiro"

ambao miguu yake iliibeba mbali sana katika sehemu za kigeni kukaa

Hapa "miguu" inawakilisha mtu mzima. "ambaye alikwenda katika sehemu za mbali kuishi na kutengeneza pesa"

iliibeba mbali sana

Hapa "iliibeba" ina maana ya mji wa Tiro ambayo inawakilisha watu wa Tiro.

Isaiah 23:8

Ni nani aliyepanga hili dhidi ya Tiro ... wa dunia?

Isaya anatumia swali kukejeli Tiro. Neno "hili" lina maana ya mipango ya Mungu kuangamiza Tiro ambayo Isaya alielezea katika 23:1-7. Pia, "Tiro" ina maana ya watu wanaoishi Tiro. Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Alikuwa Yahwe ambaye alipanga kuangamiza watu wa Tiro ... wa dunia"

mtoaji wa taji

Hapa "taji" ina maana ya nguvu ambayo mtu anayo kama mtawala juu ya watu. "ambaye huwapa watu nguvu ya kutawala juu ya wengine"

ambao wafanya biashara wake ni wakuu

Wafanya biashara wanalinganishwa na wakuu kusisitiza jinsi walivyo na nguvu walipokwenda katika nchi tofauti. "ambao wafanya biashara wao ni kama wakuu"

ambao wauzaji wake wanaheshimika katika dunia

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ambao wauzaji wake watu wa dunia wanatoa heshima kubwa zaidi"

kupunguza kiburi chake na utukufu wake wote

"kutowaheshimu kwa sababu walikuwa na kiburi kwa utukufu wao wenyewe"

kiburi chake ... utukufu wake ... walioheshimiwa wa kwake

Hapa "kwake" ina maana ya mji wa Tiro ambao unawakilisha watu wanaoishi kule. "kiburi chao .. utukufu wao ... walioheshimiwa wa kwao"

Isaiah 23:10

Lima nchi yako, kama mtu alimavyo Nile, binti wa Tarshishi. Hakuna tena soko ndani ya Tiro

Maana zaweza kuwa 1) Isaya anawaambia watu wa Tarshishi kuanza kupanda mazao kwa kuwa hawawezi tena kufanya biashara na Tiro au 2) Isaya anawaambia watu wa Tarshishi ya kuwa wapo huru kutoka na utawala wa Tiro."Pita katika nchi kama mto, binti wa Tarshishi. Watu wa Tiro hawana nguvu yoyote tena"

binti wa Tarshishi

"Binti" wa mji inawakilisha watu wa mji. "watu wa Tarshishi" au "watu ambao wanaishi Tarshishi"

Yahwe amenyosha mkono wake juu ya bahari, na ametikisa falme

Yahwe kutumia nguvu yake kuongoza bahari na watu wenye falme zenye uwezo inazungumziwa kana kwamba Yahwe alinyosha mkono wake na kutikisa falme.

amenyosha mkono wake juu ya bahari

Hapa "mkono" ina maana ya nguvu na uongozi wa Mungu. "ameonyesha nguvu yake juu ya bahari"

bikira binti wa Sidoni uliyekandamizwa

Hapa "binti bikira" inawakilisha watu wa Sidoni. "watu wa Sidoni, kwa sababu watu wengine watakukandamiza"

Isaiah 23:13

Tazama nchi ya Wakaldayo

"Wakaldayo" ni jina lingine la Wababeli. "Tazama kile kinachotokea kwa nchi ya Wababeli" au "Tazama kile kinachotokea kwa Babeli"

minara ya kuzingira

Wanajeshi walijenga minara au matuta ya udongo kushambulia juu ya kuta za mji

Lia kwa uchungu, enyi meli za Tarshishi

Hapa "meli" inawakilisha wanamume katika meli.

kwa maana kimbilio lenu limeangamizwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "kwa maana maadui wameangamiza kimbilio lako"

Isaiah 23:15

Katika siku hiyo

Hapa "siku" inawakilisha kipindi cha muda kwa ujumla. "Katika kipindi hicho" au "Pale"

Tiro itasahaulika kwa miaka sabini

Kwa kuwa watu hawatakwenda tena Tiro kununua au kuuza bidhaa, itakuwa kana kwamba wamesahau kuhusu mji ule. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "kwa miaka sabini itakuwa kana kwamba watu wamesahau kuhusu Tiro"

kwa miaka sabini

"kwa miaka 70"

kama siku za mfalme

Hapa "siku" inawakilisha kipindi kirefu zaidi cha muda. Muda wa wastani ambao mfalme aliishi ulikuwa kama miaka 70. "kama miaka ya mfalme" au "ambao ni kama urefu ambao mfalme huishi"

kama katika wimbo wa kahaba ... ili kwamba uweze kukumbukwa

Hii inazungumzia kuhusu watu wa Tiro kana kwamba walikuwa kahaba. Kama vile kahaba ambaye sio maarufu tena anaweza kuimba katika mitaa kurudisha wapenzi wake wa zamani, watu wa Tiro watajaribu kutafuta watu kutoka mataifa mengine kurudi kwao kuendelea kufanya biashara ili kwamba watu wa Tiro wawe matajiri na wenye uwezo tena.

ili kwamba uweze kukumbukwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ili kwamba watu wakukumbuke" au "ili kwamba watu warudi kwako"

Isaiah 23:17

Itakuja kuwa ya kwamba

Msemo huu unatumika hapa kuweka alama ya tukio muhimu ambalo litatokea.

miaka sabini

"miaka 70"

Yahwe ataisaidia Tiro

Hapa "Tiro" inawakilisha watu ambao wanaishi Tiro. "Yahwe atawasaidia watu wa Tiro"

ataanza kupata pesa tena kwa kufanya kazi ya ukahaba ... wa dunia

Isaya analinganisha watu wa Tiro na kahaba. Kama vile kahaba anavyojiuza kwa ajili ya pesa kwa mwanamume yeyote, watu wa Tiro watanunua na kuuza tena kwa falme zote."Na kama kahaba watanunua na kuuza na falme zote za duniani"

Haitatunzwa au kuwekwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Wafanya biashara hawatatunza pembeni pesa yao"

Wale wanaoishi ndani ya uwepo wa Yahwe

"Wale wanaomtii na kumtumikia Yahwe"

kwa ajili yao kula na kuwa na mavazi ya kudumu

"kwa wao kupata chakula cha kutosha kwa kula na nguo ambazo zitadumu muda mrefu"

Isaiah 24

Isaiah 24:1

kufanya dunia kuwa tupu

"kufanya dunia kuwa na ukiwa" au "kuangamiza kila kitu juu ya dunia"

Itakuja kuwa ya kwamba

Msemo huu unaweka alama kwa tukio muhimu.

kama itakavyokuwa ... ndivyo itakuwa

Kile Yahwe atakachofanya hakielezwi hapa, lakini kinaeleweka. Hiii inaonyesha ya kwamba Mungu atawafanya watu kw njai moja. "kama Yahwe anavyotawanya ... kw hiyo atatawanya"

kuhani ... mtoaji wa riba

Katika 24:2 Isaya anaorodhesha madaraja ya watu. Yanaweza kuwekwa kama nomino za wingi. "makuhani ... wale ambao hutoa riba"

mpokeaji wa riba

"yule ambaye hudaiwa fedha". Neno "riba" lina maana ya fedha ya ziada ambayo mtu anatakiwa kulipa ili aweze kukopa fedha.

mtoaji wa riba

"yule ambaye anadaiwa fedha"

Isaiah 24:3

Dunia itaharibiwa kabisa na kuvuliwa kabisa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe atahariibu kabisa dunia na ataondoa kila kitu chenye thamani"

Yahwe amanena neno hili

Hapa "neno" linawakilisha kile Yahwe alichosema. "Yahwe amesema angefanya"

Dunia inakauka na kunyauka, dunia inakauka na kutokomea

Misemo hii miwili ina maana moja. "Kila kitu juu ya dunia kitakauka na kufa"

Dunia ... ulimwengu

Zote hizi zinawakilisha kila kiitu ambacho kipo juu ya dunia.

Dunia inachafuliwa na wakazi wake

Watu kutenda dhambi na kufanya dunia kutokubalika kwa Mungu inazungumziwa kana kwamba watu walifanya dunia kuwa chafu kimwiili. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Watu wamechafua dunia"

wamevunja sheria, kukiuka amri, na kuvunja agano la milele

"hawajatii sheria na amri za Mungu, na wamevunja agano la milele la Mungu"

Isaiah 24:6

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kufafanua kipindi katika siku za usoni ambapo Mungu atahukumu dunia. Manabii mara nyingine hufafanua tukio la siku za usoni kama kitu cha nyuma au cha sasa. Hii inasisitiza tukio kufanyika kwa uhakika.

laana humeza dunia

Yahwe kulaani dunia na kuiangamiza inazungumziwa kana kwamba laana ilikuwa aidha mnyama pori ambaye anakula kabisa dunia au moto ambao huchoma kabisa dunia.

na wakazi wake wanakutwa na hatia

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "na Yahwe atatamka ya kwamba watu wana hatia"

Isaiah 24:8

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kufafanua kipindi katika siku za usoni ambapo Mungu atahukumu dunia. Manabii mara nyingine hufafanua tukio la siku za usoni kama kitu cha nyuma au cha sasa. Hii inasisitiza tukio kufanyika kwa uhakika.

vigoma ... kinubi

Hivi ni vyombo vya muziki.

Isaiah 24:10

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kufafanua kipindi katika siku za usoni ambapo Mungu atahukumu dunia. Manabii mara nyingine hufafanua tukio la siku za usoni kama kitu cha nyuma au cha sasa. Hii inasisitiza tukio kufanyika kwa uhakika.

Mji wa uharibifu umevunjwa chini

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe atavunja chini mji wa uharibifu"

Mji wa uharibifu

Maana zaweza kuwa 1) mji ulikuwa katika uharibifu kabla Mungu hajauvunja chini; watu hawakumtii Mungu, serikali ilikuwa imeharibika, na mji ulikuwa umejaa unywaji na sherehe, au 2) mji utakuwa katika uharibifu baada ya Mungu kuuvunja chini. Kuta na majengo ambayo hapo awali yalikuwa na nguvu na marefu sasa yapo katika uharibifu juu ya ardhi. Kwa maana zote mbili, ina maana ya miji kwa ujumla na sio mji mmoja.

kila nyumba inafungwa na kuwa tupu

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "watu watafunga nyumba zo na kuziacha tupu"

kwa sababu ya mvinyo

"kwa sababu hakuna divai"

furaha yote inawekwa giza, shangwe ya nchi imepotea

Misemo hii miwili ina maana moja. "furaha yote itaondoka kutoka duniani"

shangwe ya nchi

Hapa "nchi" inawakilisha watu wa dunia.

Isaiah 24:12

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kufafanua kipindi katika siku za usoni ambapo Mungu atahukumu dunia. Manabii mara nyingine hufafanua tukio la siku za usoni kama kitu cha nyuma au cha sasa. Hii inasisitiza tukio kufanyika kwa uhakika.

Ndani ya mji kunaachwa ukiwa

Nomino dhahania "ukiwa" inaweza kuandikwa kama "tia ukiwa" au "tupu". "Mji umetiwa ukiwa" au "Mji umeachwa tupu"

Ndani ya mji

Huu sio mji mmoja lakini miji kwa ujumla.

kama pale mzeituni unapigwa, kama vile masazo ya mavuno baada ya mavuno ya zabibu kukamilika

Hii inalinganisha mataifa baada ya Yahwe kuharibu nchi kwa miti na mizabibu baada ya matunda kuchukuliwa. Hii ina maana kutakuwa na watu wachache sana waliosalia katika nchi.

Isaiah 24:14

Watainua juu sauti zao na kupiga kelele utukufu wa Yahwe

Msemo "inua juu sauti zao" ni lahaja ambayo ina maana ya kuongea kwa sauti kubwa. "Wataimba na kupiga kelele kuhusu utukufu wa Yahwe"

Wata

Hapa "wata" ina maana ya wale ambao bado wapo hai baada ya Yahwe kuharibu dunia.

na watapiga kelele kwa shangwe kutoka baharini

Hapa "bahari" ina maana ya Bahari ya Mediteranea ambayo ipo magharibi mwa Israeli. "na wale wa magharibi kuelekea bahari watapiga kelele za shangwe"

Kwa hiyo katika mashariki mtukuze Yahwe

Msemo "katika mashariki" inawakilisha watu wanaoishi mashariki mwa Israeli. Isaya anaamuru watu hawa kana kwamba walikuwa plae pamoja naye. Lakini, anazungumza na watu katika siku za usoni baada ya Mungu kuharibu dunia. "Kwa hiyo kila mtu kutoka nchi za mbali za mashariki watamtukuza Yahwe"

na katika visiwa vvya bahari mpatie utukufu

Isaya anawaamuru watu ambao wanaishi katika visiwa katika bahari ya Meditarenea kana kwamba walikuwa pale pamoja naye. Lakini, anazungumza kwa watu katika siku za usoni baada ya Mungu kuharibu dunia. "na kila mtu katika visiwa atatoa utukufu

kwa jina la Yahwe

Hapa "jina" inawakilisha Yahwe. "kwa Yahwe"

Isaiah 24:16

tumesikia

Hapa "tumesikia" ina maana ya Isaya na watu wa Israeli. Isaya anafafanua kitu katika siku za usoni kana kwamba kimekwisha tokea. "tutasikia"

Nimeisha, nimeisha

Isaya anarudia msemo huu kusisitiza uchungu wake. Alijihangaisha sana kwa sababu aliwaona watu ambao walidanganya wengine na hawakufanya kile walichoahidi kufanya. "Nimekuwa dhaifu sana"

Wadanganyifu wamefanya udanganyifu; ndio, wadanganyifu wamefanya udanganyifu

Isaya anarudia msemo huu kusisitiza uchungu wake. "Kweli, wale ambao hudanganya sasa wanadanganya wengine" au "Kweli, wadanganyifu wametenda udanganyifu"

Isaiah 24:17

Hofu kuu, shimo, na mtego upo juu yako, wakazi wa dunia

"Nyie watu wa dunia mtapitia hofu kuu, shimo, na mtego"

shimo, na mtego ... atakamatwa katika mtego

Hapa "shimo" na "mtego" inawakilisha mambo mabaya yote tofauti ambayo yatatokea kwa watu. Watu watatoroka kitu kimoja kibaya lakini watapitia kitu kingine kibaya.

sauti za hofu kuu

"sauti ya kutisha"

atakamatwa katika mtego

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "mtego utamkamata"

Madirisha ya mbinguni yatafunguliwa

Hii inazungumzia kiasi kikubwa cha mvua kunguka kutoka angani kana kwamba Yahwe alifungua dirisha katika anga na kuruhusu maji kumwagika. "Anga itafunguka wazi na mvua nyingi itamwagika"

misingi ya dunia itatikisika

Neno "msingi" kawaida lina maana ya umbo la mawe ambalo hutoa mhimili kwa jengo kutok kwa chini. Hapa inaelezea umbo la kufanana ambalo lilidhaniwa kushikilia dunia katika sehemu yake. "dunia itatikisika kwa kutisha" au "kutakuwa na tetemeko la kutisha"

Isaiah 24:19

Dunia itavunjwa kabisa, dunia itararuliwa kabisa; dunia itatikiswa kwa nguvu

Vishazi hivi vinaweza kuwa katika hali ya kutenda. "Dunia itavunjika na kugawanyika; dunia itatikisika kwa nguvu"

Dunia itapepesuka kama mwanamume mlevi na itayumba huku na kule kama kibanda

Tashbihi hizi zinasisitiza jinsi dunia itakavyotikisa huku na kule.

Dhambi yake itakuwa nzito juu yake na itaanguka na haitainuka tena

Hii inazungumzia dunia kana kwamba ilikuwa mtu na wadanganyifu walikuwa vyombo vizito. Mtu hujaribu kubeba mzigo mzito lakini uzito unasababisha mtu kunguka na kutoweza kusimama juu. Hapa dunia inawakilisha watu wa dunia ambao husababisha Yahwe kuangamiza dunia kwa sababu ya dhambi zao. "Dhambi za watu ni nyingi na kwa hiyo Yahwe ataangamiza dunia, na dunia itakuwa kama mtu ambaye huanguka na hawezi kusimama juu"

Isaiah 24:21

Itakuja kuwa

Hii inaweka alama kwa tukio muhimu.

katika siku hiyo

Hapa "siku" ina maana ya kipindi cha muda kwa ujumla. "katika kipindi hicho"

wingi wa walio juu

Msemo "wingi" au "jeshi" ni neno ambalo lina maana ya idadi kubwa ya kitu. Hapa ina maana ya viumbe viovu vya kiroho katika mbingu. "viumbe viovu vya kiroho" au "malaika ambao waliasi dhidi yake"

walio juu

Hapa "juu" inawakilisha mbinguni au anga. "katika mbingu" au "katika anga"

Watakusanywa pamoja, wafungwa katika shimo, na watafungwa katika gereza

Hapa "shimo" ina maana ya chumba chenye giza au shimo katika gereza. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe atawakusanya pamoja kama wafungwa wake na kuwafunga katika gereza la chini"

wataadhibiwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe atawaadhibu"

Kisha mwezi utaaibishwa, na jua kufedheheshwa

Jua na mwezi inaelezwa kama mtu ambaye anaona aibu ya kuwa mbele ya mtu mwenye nguvu kubwa. Katika uwepo wa Yahwe, nuru ya mwezi na jua itaonekana na mwanga mdogo.

Isaiah 25

Isaiah 25:1

nitasifu jina lako

Hapa "jina" inawakilisha Yahwe. "ninakusifu"

vitu vilivyopangwa zamani

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "vitu ulivyovipanga zamani"

katika uaminifu kamilifu

Nomino dhahania "uaminifu" inaweza kuwekwa kama "mwaminifu". "kwa sababu wewe ni mwaminifu uliye mkamilifu"

mji ule

Hii haimaanishi mji fulani. Ina maana na miji kwa ujumla.

ngoma ya wageni

"ngome ambayo ni ya wageni"

mji wa mataifa katili

Hapa "mji" na "mataifa" inawakilisha watu ambao wanaishi pale.

Isaiah 25:4

umekuwa sehemu ya usalama ... hifadhi ... hifadhi kutoka kwa dhoruba ... kivuli kutoka kwa joto

Yahwe kuwalinda watu wake inazungumziwa kana kwamba alikuwa sehemu ambayo watu wanaweza kwenda kuwa salama na kufarijiwa.

Pale ambapo pumzi ya wakatili ulipokuwa kama dhoruba dhidi ya ukuta

Watu wakatili kuwakandamiza watu wa Mungu inazungumziwa kana kwamba walikuwa dhoruba inayopiga dhidi ya ukuta.

Pale ambapo pumzi

"Pale upepo" au "Pale mlipuko"

wakatili

Hiki ni kitenzi kidogo."watu wakatili" au "wale ambao ni wakatili"

kama joto katika nchi kavu

Hii inalinganisha adui wa watu wa Mungu kwa joto ambalo hukausha nchi. Hii inasisitiza jinsi maadui wanavyosababisha watu wa Mungu kuteseka.

kama joto linapotulizwa ... wakatili unajibiwa

Yahwe kuwasimamisha watu wakatili kutokuimba na kujivuna inalinganishwa na wingu kutoa kivuli katika siku ya kiangazi. Hii inasisitiza ya kwamba Yahwe huwafariji watu wake kwa kusimamisha wale ambao husababisha wao wateseke.

kama vile joto linavyotulizwa kwa kivuli cha wingu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "kama vile wingu linavyopita juu kichwani na kutuliza joto"

wimbo wa wakatili unajibiwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "utawazuia watu wakatili kutokuimba"

Isaiah 25:6

Katika mlima huu

Hii ina maana ya Yerusalemu au Mlima Sayuni.

Yahwe wa majeshi

Yahwe wa majeshi ya Israeli.

karamu ya vitu vinono

Hapa "vitu vinono" ina maana ya vyakula bora.

karamu katika masimbi

"divai ya zamani". Hii ina maana ya divai bora.

kifuniko juu ya watu wote, utando ulifumwa juu ya mataifa

Kifo, mateso, na huzuni inazungumziwa kana kwamba vilikuwa wingu jeusi au utando ambao hufunika kila mtu juu ya dunia.

Ataimeza mauti milele

Yahwe kusababisha watu kuishi milele inazungumziwa kana kwamba angeweza kumeza kifo.

aibu ya watu wake ataiondoa kutoka dunia nzima

Yahwe kusababisha watu kutokuwa na aibu tena inazungumziwa kana kwamba aibu ilikuwa kitu ambacho Yahwe angeweza kuondoa mbali.

Isaiah 25:9

Itasemwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Watu watasema"

katika siku hiyo

Hapa "siku" inawakilisha kipindi cha muda kwa ujumla. "katika kipindi hicho"

Kwa kuwa katika mlima huu mkono wa Yahwe utapumzika

"mkono" unawakilisha nguvu ya Mungu. Kwa maana mkono wa Yahwe kupumzika juu ya "mlima huu" ina maana atawalinda watu wake. "Nguvu ya Yahwe itakuwa juu ya mlima huu" au "Kwa maana juu ya Mlima Sayuni Yahwe atalinda watu wake"

Moabu itakanyagwa chini katika nafasi yake, hata kama majani makavu yanavyokanyagwa chini katika shimo lililojaa mbolea

Yahwe kuangamiza watu wa Moabu inazungumziwa kana kwamba angewakanyaga na kuwasaga. Hii inalinganishwa na jinsi watu wanavyokanyaga majani makavu kuchanganya na mbolea.

Moabu itakanyagwa chini katika nafasi yake

Hapa Moabu anawakilisha watu wa Moabu. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Yahwe atakanyaga watu wa nchi ya Moabu"

Isaiah 25:11

Watatawanya mikono yao ... mikono yake kuogelea

Tashbihi hii inasisitiza jinsi gani Yahwe atawaibisha watu wa Moabu. Watatawanya mikono yao katika kinyesi cha mnyama kama mwogeleaji anavyotawanya mikono yake majini.

Watatawanya mikono yao katikati yake

"Watu wa Moabu watasukuma mikono yao katikati ya kinyesi cha mnyama"

kama mwogeleaji anavyotawanya mikono yake kuogelea

"kana kwamba walikuwa wakiogelea"

atashusha chini kiburi chake

Yahwe kuaibisha mtu mwenye kiburi inazungumziwa kana kwamba kiburi ilikuwa kitu cha juu na Yahwe angekisababisha kuwa chini.

pamoja na ujuzi wa mikono yao

Hapa "mikono" inawakilisha nguvu ya kufanya au kutengeneza kitu. "pamoja na vitu vikubwa walivyotengeneza" au "pamoja na vitu vikubwa walivyofanya"

ngome yako ya juu ya kuta atazishusha chini mpaka kwenye ardhi, kwenye vumbi

Hii inazungumzia Yahwe kusababisha majeshi kuzileta chini kuta kana kwamba yeye mwenyewe alikuwa akienda kuzileta chini. "Atatuma jeshi kuleta ngome yako iliyo juu ya kuta ardhini, katika mavumbi"

Ngome yako ya juu

Hapa "yako" ina maana ya watu wa Moabu. Inaweza kuwekwa katika mtu wa tatu kuwe na mlingano na mstari uliopita. "Ngome yao iliyo juu"

Isaiah 26

Isaiah 26:1

Katika siku hiyo

Hapa "siku" inawakilisha kipindi cha muda kwa ujumla. "Katika kipindi hicho"

wimbo huu utaimbwa katika nchi ya Yuda

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "watu katika nchi ya Yuda wataimba wimbo huu"

Tuna mji imara

Hii ina maana ya mji wa Yerusalemu.

Mungu amefanya wokovu ukuta na boma lake

Nguvu ya Mungu kuwalinda na kuwaokoa watu wake inazungumziwa kana kwamba wokovu wake ulikwa ukuta unaozunguka mji.

taifa lenye haki linaloshikilia imani

Hapa "taifa" inawakilisha watu. "watu wenye haki na waaminifu"

Isaiah 26:3

Akili ambayo imekaa kwako

Hapa "akili" inawakilisha mawazo ya mtu. Pia, "kwako" ina maana ya Yahwe. Msemo "Akili ambayo imekaa kwako" ni lahaja ambayo ina maana "Mtu ambaye huwaza kwa kuendelea juu yako"

Yah, Yahwe

Yah ni jina lingine kwa ajili ya Yahwe.

Yahwe, ni mwamba wa milele

Yahwe kuwa na nguvu ya kuwalinda watu wake inazungumziwa kana kwamba alikuwa jiwe refu ambapo watu wanaweza kwenda kutoroka maadui zao.

Isaiah 26:5

atawashusha chini wale ambao wanaishi kwa kujiinua

Yahwe kuwaaibisha wale ambao wanajiinua inazungumziwa kana kwamba watu wenye kiburi walikuwa juu na angeweza kusababisha washuke chini.

miji iliyoimarishwa

Hii ina maana miji iliyoimarishwa kwa ujumla sio mji fulani.

ataiweka chini ... atasambaratisha

Yahwe kusababisha jeshi kuangamiza miji iliyoimarishwa inazungumziwa kana kwamba yahwe angefanya mwenyewe.

itakanyagwa chini kwa miguu ya maskini na kutembea kwa wahitaji

Kauli mbili zina maana moja. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Maskini na watu walioteswa watakanyaga juu ya uharibifu wa mji"

Isaiah 26:7

Njia ya wenye haki ina usawa ... njia ya wenye haki umefanya iwe wima

Misemo hii miwili ina maana moja. Watu kumtii Yahwe inazungumziwa kana kwamba walikuwa wakitembea juu ya njia yake. Yahwe kuhakikishia watu ya kwamba kile wanachofanya ni sahihi inazungumziwa kana kwamba alikuwa akifanya njia kuwa sawa na wima kwa ajili yao.

katika njia ya hukumu zako, Yahwe, tunakusubiri

Kufanya kile Yahwe amehukumu kuwa sahihi inazungumziwa kutembea katika njia yake. "tunakusubiri, Yahwe, tunapoendelea kufanya kile ulichohukumu kuwa sahihi"

ya hukumu zako

"ya sheria zako" au "ya mafundisho yako"

tunakusubiri

Hapa "tunakusubiri" ina maana ya Isaya na watu wote wenye haki ambao wanazungumza na Yahwe.

jina lako na sifa yako ni shauku yetu

Hapa "jina" na "sifa" inawakilisha silika ya Yahwe ambayo inawakilisha Yahwe mwenyewe. "shauku yetu pekee ni kukuheshimu"

roho yangu ndani yangu inakutafuta kwa bidii

Kutaka kumjua Yahwe na sheria zake zaidi inazungumziwa kana kwamba mtu alikuwa akitaka kumtafuta Yahwe. "Ninataka kukujua zaidi kwa bidii"

roho yangu ndani yangu inakutafuta kwa bidii

Hapa "roho" inawakilisha msemaji kwa yeye mzima.

Isaiah 26:10

Acha fadhila ionyeshwe kwa mtu muovu, lakini hatajifunza haki

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Hata kama Yahwe ni mwema kwa watu waovu, bado hawajifunzi kufanya kile kilicho sahihi"

mtu muovu

Hii ina maana watu waovu kwa ujumla.

katika nchi ya wenye haki

Hapa "nchi" inawakilisha watu ambao wanaishi kule. "Katika nchi ambapo watu hufanya kile kilicho sahihi"

haoni ukuu wa enzi wa Yahwe

Hapa "kuona" inawakilisha kutambua kitu. "hatambui ya kwamba Yahwe ni mkuu"

Isaiah 26:11

mkono wako umeinuliwa juu

Yahwe kujiandaa kuwaadhibu watu waovu inazungumziwa kana kwamba mkono wake uliinuliwa na unataka kuwapiga watu waovu.

lakini hawagundui

"lakini watu waovu hawagundui"

wataona ari yako kwa ajili ya watu

Hapa "kuona" inawakilisha kugundua kitu. "watagundua ya kwamba una hamu ya kuwabariki watu wako"

kuaibishwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "wataaibishwa"

moto wa adui zako utawaangamiza

Yahwe kuwaadhibu na kuwaangamiza kabisa adui zake inazungumziwa kana kwamba angetuma moto ambao utawachoma kabisa.

moto wa adui zako

Hapa "wa" haimaanishi moto ni wa maadui lakini ya kwamba moto umekusudiwa kutumiwa dhidi ya maadui. "moto wako utawachoma kabisa"

kwa ajili yetu

Hapa "yetu" ina maana ya Isaya na inajumlisha watu wote wenye haki.

Isaiah 26:13

lakini tunasifu jina lako pekee

Hapa "jina" inawakilisha nafsi ya Mungu. "lakini tunakusifu wewe peke yako"

hawatainuka

"hawatarudi katika uhai"

kufanya kila kumbukumbu yao kutoweka

Yahwe kusababisha watu kutokumbuka wale aliowaangamiza inazungumziwa kana kwamba Yahwe alifanya kumbukumbu yao kutoweka au kufa.

Isaiah 26:15

Umeongeza taifa, Yahwe, umeongeza taifa

Kishazi hiki kinarudiwa kwa ajili ya msisitizo. Hapa "taifa" inawakilisha watu. "Umeongeza sana idadi ya watu katika taifa letu"

Isaiah 26:16

walikuangalia wewe

Hapa "walikuangalia" ina maana ya watu wa Israeli. Hii ingeweza kujumuisha Isaya. "tuliangalia kwako"

walikuangalia wewe

Lahaja hii ina maana walimuuliza Yahwe kwa msaada.

nidhamu yako ilipokuwa juu yao

Nomino dhahania "nidhamu" inaweza kuwekwa kama kitenzi. "unapowaadhibisha"

Kama mwanamke mwenye mimba .. anapolia katika maumivu yake ya uchungu

Hii inalinganisha watu kwa mwanamke kuzaa. Hii inasisitiza mateso na kulia kwao Yahwe alipowaadhibisha"

Isaiah 26:18

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kulinganisha mateso ya watu wa Yuda na mwanamke anayezaa.

lakini ni kana kwamba tumezaa tu upepo

"lakini ni kana kwamba tumezaa tu hewa" au "ni kana kwamba tumezaa utupu".Hii ni tashbihi ambayo inasisitiza ya kwamba mateso ya watu hayajaleta kitu chochote. "lakini hakuna kitu kizuri kilichotokana kwake"

Hatujaleta wokovu katika dunia, na wakazi wa ulimwengu hawajaanguka

Hapa "dunia" inawakilisha watu ambao wanaishi juu ya dunia. Maana haiko wazi, lakini inaonekana kumaanisha ya kwamba watu wa Israeli hawakuweza kujiokoa wenyewe au watu wengine kwa kuwashinda adui zao vitani.

Hatujaleta wokovu katika dunia

Hii inaweza kuandikwa upya ili kwamba nomino dhahania "wokovu" ielezwe kama kitenzi "kuokoa". "Hatujaokoa wakazi wa dunia"

na wakazi wa ulimwengu hawajaanguka

"wala hatujasababisha watu waovu wa ulimwengu kuanguka katika vita"

Isaiah 26:19

Wafu wako wataishi

Hii inawezwa kuandikwa upya ili kwamba kivumishi kidogo "wafu" kinaelezwa kama kitenzi "wamekufa". "Watu wako ambao wamekufa wataishi tena"

Wafu wako

Maana zaweza kuwa 1) "wako" ina maana ya Yahwe au 2) "Wako" ina maana ya watu wa Israeli. Iwapo utachagua chaguo la pili unaweza kutafsiri kama "Wafu wetu"

Inukeni

Hii inazungumzia watu waliokufa kurudi katika uhai kana kwamba walikuwa wakiamka kutoka usingizini.

nyie mnaoishi katika vumbi

Hii ni njia ya upole ya kumaanisha wale waliokufa. "wale ambao wamekufa na kuzikwa"

kwa maana umande wako ni umande wa mwanga

Yahwe kuwa mwema kwa watu wake na kuwaleta katika uhai inazungumziwa kana kwamba ilikuwa umande ambao unasababisha mimea kuishi.

kwa maana umande wako

Maana zaweza kuwa 1) "wako" ina maana ya Yahwe na huu ni umande ambao Yahwe hutoa au 2) "wako" ina maana ya watu wa Israeli na huu ni umande wanaopata kutoka kwa Yahwe.

umande wa mwanga

Maana zaweza kuwa 1) "mwanga" ina maana ya nguvu ya Yahwe kufanya watu waliokufa kuishi tena. "umande kutoka kwa Yahwe" au 2) "mwanga" ina maana ya kipindi cha asubuhi ambapo umande upo juu ya mimea. "umande wa asubuhi"

dunia italeta mbele wafu wake

"dunia itazaa wale waliokufa". Yahwe kusababisha watu waliokufa kuja katika uzima inazungumziwa kana kwamba dunia ingeweza kuzaa wale waliokufa. "na Yahwe atasababisha wale ambao wamekufa kuinuka kutoka katika dunia"

Isaiah 26:20

watu wangu

Hapa "wangu" ina maana ya Isaya. Pia "watu" ina maana ya watu wa Israel.

hadi pale hasira itakapopita

"hadi Yahwe atakapokuwa hana hasir ana sisi tena"

dunia itafunua damu yake, na haitaficha tena waliouwawa wa kwake

Yahwe kufunua mauaji yote ambayo yamefanyika duniani ili kwamba aweze kuadhibu inazungumziwa kana kwamba dunia yenyewe itamfunua kila mmoja ambaye alikuwa ameuawa.

Isaiah 27

Isaiah 27:1

Katika siku hiyo

Hapa "siku" inawakilisha kipindi cha muda kwa ujumla.

Yahwe kwa mkono wake, kwa upanga mkubwa na mkali ataadhibu

Yahwe kuwa na nguvu ya kuangamiza adui zake inazungumziwa kana kwamba alikuwa na upanga imara, na mkubwa.

jitu la kutisha ambalo limo katika bahari

Hii ina maana ya Lewiathani

Shamba la mizabibu la mvinyo, litaimba kwa ajili yake

"Imba juu ya shamba la mizabibu la mvinyo".Hii inazungumzia kuhusu watu wa Israeli kana kwamba walikuwa shamba la mizabibu ambalo lilizaa matunda. "Imba kuhusu watu wa Israeli kana kwamba walikuwa shamba la mizabibu ambalo lilizaa mizabibu kwa ajili ya mvinyo"

Mimi, Yahwe, ni mlinzi wake

"Mimi, Yahwe, hulinda shamba la mizabibu"

usiku na mchana

Maneno "usiku" na "mchana" yanaunganishwa hapa kumaanisha "wakati wote". "wakati wote" au "kwa kuendelea"

Isaiah 27:4

Kauli Kiunganishi

Hii inaendelea kuzungumza kuhusu watu wa Israeli kana kwamba walikuwa shamba la mizabibu.

Sina hasira, Oh, hata kuwe na mibigili na miiba! Katika vita nitatembea dhidi yao

"Sina hasira. Kama kulikuwa na mibigili na miiba ningetembea dhidi yao katika vita"

Sina hasira

Inaeleweka ya kwamba Yahwe hana hasira na watu wake tena. "Sina hasira na watu wangu tena"

hata kuwe na mibigili na miiba

Adui za watu wa Israeli wanazungumziwa kana kwamba walikuwa mibigili na miiba inayoota katika shamba la mizabibu.

mibigili na miiba

Mibigili na miiba hutumika mara kwa mara kama alama ya miji na nchi zilizoharibiwa

Katika vita nitatembea dhidi yao

Yahwe kupigana na adui zake inazungumziwa kana kwamba alikuwa mwanajeshi katika jeshi.

Ningetembea dhidi yao; Ningewachoma wote kwa pamoja

Hapa Isaya anaunganisha picha tofauti kuzungumzia maadui wa Yahwe. Anazungumza juu yao kana kwamba walikuwa mibigili na miiba lakini pia kama wanajeshi katika jeshi.

isipokuwa washike ulinzi wangu

Hii inaweza kuandikwa upya ili kwamba nomino dhahania "ulinzi" ielezwe kama kitenzi "kulinda". "Isipokuwa waniulize kuwalinda wao"

na kufanya amani pamoja na mimi; waache wafanya amani pamoja na mimi

"na waombe kuishi kwa amani pamoja nami; ninataka waishi kwa amani pamoja nami"

Isaiah 27:6

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza. Anaendelea kufafanua watu wa Israeli kama shamba la mizabibu.

Katika siku ijayo

Hii inazungumza juu ya siku kana kwamba inasafiri na kufika sehemu. "Katika siku za usoni"

Yakobo atachuku mzizi; Israeli atachanua na kuchomoza

Yahwe kubariki watu wa Israeli na kusababisha waweze kufanikiwa inazungumziwa kana kwamba walikuwa mzabibu unaota mizizi na kuchanua. "uzao wa Israeli utafanikiwa kama mzabibu ambao umeshika mizizi na kuchanua"

Yakobo ... Israeli

Hapa "Yakobo" na "Israeli" ni mfano wa maneno ambao yanawakilisha uzao wa Yakobo.

watajaza uso wa nchi kwa matunda

Yahwe kusababisha watu wa Israeli kufanikiwa sana ili kwamba waweze kuwasaidia watu wengine inazungumziwa kana kwamba walikuwa mzabibu ambao huotesha matunda mengi sana hadi kufunika dunia.

Isaiah 27:7

Je! Yahwe amemshambulia Yakobo na Israeli kama alivyoshambulia mataifa ambayo yaliwashambulia?

Swali linatumika kutofautisha ukali wa adhabu ya Mungu. "Yahwe kwa uhakika aliadhibu adui wa mataifa zaido na alivyoadhibu watu wa Israeli"

Yakobo ... Israeli

Haya yanawakilisha vizazi vya Yakobo.

Je! Yakobo na Israeli wameuwawa kama katika kuchinja kwa mataifa yale ambayo yaliuwawa na wao?

Swali hili pia linatumika kutofautisha ukali wa adhabu ya Mungu. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Yahwe hajawaua watu wa Israeli kama alivyowaua adui zake kutoka kwa mataifa mengine"

Kwa kipimo sahihi umepambana

Hapa "umepambana" ina maana ya Mungu. Yahwe kuadhibu watu wake kama walivyohitaji inazungumziwa kana kwamba adhabu ya Mungu ilikuwa kity ambacho kiliweza kupimwa. "Lakini uliwaadhibu kama ilivyohitajika"

kuwatuma mbali Yakobo na Israeli

Hii inawakilisha uzao wa Yakobo "kuwatuma Waisraeli mbali"

aliwafukuza mbali kwa upepo wake mkali, katika siku ya upepo wa mashariki

Nguvu ya Yahwe kuwatuma watu wake mbali katika nchi ya kigeni inazungumziwa kana kwamba Yahwe alitumia upepo kuwapuliza mbali mpaka nchi ya kigeni. "nguvu ya Yahwe kuwaendesha nje kama upepo mkali kutoka mashariki"

Isaiah 27:9

Kwa hiyo kwa njia hii

Maana zaweza kuwa 1) "hii" ina maana ya Yahwe kuwatuma watu uhamishoni kama Isaya alivyosema katika mstari uliopita au 2) "hii" ina maana ya matendo ambay Isaya atayataja katiika sehemu inayofuata ya mstari wa 9.

udhalimu wa Yakobo utalipiwa kosa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe ataondoa dhambi kutoka kwa Waisraeli" au "Yahwe atasamehe dhambi ya Waisraeli"

udhalimu wa Yakobo ... kuondolewa kwa dhambi yake

Hapa "Yakobo" inawakilisha uzao wa Yakobo. "udhalimu wa Waisraeli ... kuondolewa kwa dhambi zao"

kwa maana hii itakuwa

Hapa "hii" ina maana ya matendo ambayo Isaya atafafanua katika sehemu inayofuata ya mstari wa 9.

tunda kamili

Hii inazungumzia matokeo ya matendo kana kwamba ilikuwa tunda ambalo huota juu ya mti au mzabibu. "tokeo"

atafanya mawe yote ya madhabahu kama chokaa na kupondwa vipande vipande, na hakuna nguzo za Ashera au ubani wa madhabahu utabaki ukisimama

Hapa "atafanya" ina maana ya Yakobo ambaye anawakilisha vizazi vyake. "Wataangamiza kabisa madhabahu yote ambayo wanatoa sadaka kwa miungu ya uongo, na watatoa sanamu zote za Ashera na madhabahu ambayo wanachoma ubani kwa miungu ya uongo"

Isaiah 27:10

Kwa maana mji ulioimarishwa una ... kumaliza matawi yake

Hapa isaya anafafanua tukio ambalo litatokea katika siku za usoni kana kwamba limeshatokea. Hii inasisitiza ya kwamba hakika litatokea.

Kwa maana mji ulioimarishwa una ukiwa, na makazi yametelekezwa na kuachwa kama nyika

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Miji ambayo ilikuwa na nguvu na ilikuwa na watu wengi wanaoishi ndani mwao itakuwa tupu kama jangwa"

mji ulioimarishwa ... makazi

Hii haimaanishi mji bayana au makazi lakini miji au makazi kwa ujumla.

ndama hula, na pale hulala chini na kumaliza

Hapa "ndama" inawakilisha ndama au ng'ombe kwa ujumla. "ndama hula, na pale wanalala chini na kumaliza"

matawi ... sio watu wenye uelewa

Watu hawa kuwa dhaifu sana kwa sababu hawamtii Yahwe ili kwamba maadui waweze kuwaangamiza kwa urahisi inazungumziwa kana kwamba walikuwa matawi makavu ambayo wanawake huvunja kutoka kwenye mti.

Matawi yatakaponyauka, yatavunjwa. Wanawake watakuja na kutengeneza moto kwao

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Matawi yatakaponyauka, wanawake watakuja na kuyavunja na kutengeneza moto nayo"

hawa sio watu wenye uelewa

Hii inaweza kuwekwa wazi zaidi. "hawa sio watu ambao wanamwelewa Yahwe au sheria yake"

watu

Maana zaweza kuwa 1) "watu" ina maana ya watu wa Israeli au 2) "watu" ina maana ya watu wa mataifa ya kigeni ambao hukandamiza watu wa Israeli.

Kwa hiyo Muumba wao hatakuwa na huruma juu yao, na yule aliyewaumba hatakuwa na rehema kwao

Vishazi hivi viwili vina maana moja. "Kwa sababu hawaelewi, Yahwe, yule aliyewaumba, hatakuwa na rehema kwao"

Isaiah 27:12

Itakuja kuwa

Msemo huu unaweka alama kwa tukio muhimu ambalo litatokea.

katika siku hiyo

Hapa "siku" inawakilisha kipindi cha muda kwa ujumla.

Yahwe atapura

Yahwe kukusanya watu wake kuwarudisha kutoka mataifa ya kigeni katika nchi ya Israeli inazungumziwa kana kwamba alikuwa akipura mtama kugawanya nafaka kutoka kwa makapi.

kutoka Mto Frati, mpaka kwenye korongo kavu la mto la Misri

Isaya anataja Mto Frati na Korongo kavu la Misri kumaanisha ya kwamba Yahwe atawarudisha watu wa Israeli ambao walikuwa uhamishoni katika nchi karibu na maji hayo, yaani, Ashuru na Misri. Mto Frati ni kaskazini mashariki mwa Israeli, na Korongo Kavu la Misri ni kusini magharibi mwa Israeli.

korongo kavu la mto la Misri

"kijito kidogo cha Misri"

wewe ... utakusanywa mmoja baada ya mwingine

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe atawakusanya mmoja mmoja"

tarumbeta kubwa itapulizwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "mtu atapulizwa tarumbeta kwa sauti"

wanaoangamia katika nchi ya Ashuru watakuja, na waliotengwa katika nchi ya Misri

Taarifa inayoeleweka inaweza kuwekwa wazi. "wale ambao wapo uhamishoni na kufa katika nchi ya Ashuru na nchi ya Misri watarudi katika nchi ya Israeli"

mlima mtakatifu

"mlima mtakatifu" ni Mlima Sayuni, katika Yerusalemu.

Isaiah 28

Isaiah 28:1

Ole wake shada la maua lenye kiburi ...juu ya kichwa cha Bonde linalositawi ya wale ambao wamezidiwa na mvinyo

"shada la maua" ni taji linalotengenezwa kwa maua. Hapa linawakilisha mji wa Samaria, mji mkuu wa Israeli, ambao upo juu ya bonde lenye rutuba. Samaria na watu wake kuangamizwa inazungumziwa kana kwamba shada la maua litazeeka na kuacha kuwa zuri.

Tazama

"Sikiliza" au "Zingatia kwa makini"

ambao wamezidiwa na mvinyo

"ambao wamelewa kwa mvinyo"

Bwana humtuma yule ambaye ana uwezo na nguvu

Hapa "yule" ina maana ya mfalme mwenye nguvu ambaye pia anawakilisha jeshi lake lenye nguvu. "Bwana hutuma mfalme pamoja na jeshi lake lenye nguvu"

dhoruba ya mvua ya mawe

"Dhoruba ya mvua ya mawe" inatokea pale ambapo vipande vigumu vya barafu kutoka angani huanguka. Hapa ni tashbihi ambayo ina maana ya jeshi la adui ambalo Yahwe atatuma kuangamiza watu wa Samaria.

atatupa kila taji la shada la maua chini katika ardhi

Mfalme na jeshi lake lenye nguvu kuangamiza watu wa Samaria na mji wao inazungumziwa kana kwamba mfalme atarusha mashada ya maua ya watu chini ardhini.

Isaiah 28:3

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza juu ya watu na mji wa Samaria kana kwamba walikuwa shada la maua.

Shada la maua lenye kiburi la walevi wa Efraimu watakanyagwa chini ya miguu

Isaya anaendelea kuzungumza juu ya watu na mji wa Samaria kana kwamba walikuwa shada la maua.

shada la maua lenye kiburi ... wa Efraimu ... ambao uko juu ya kichwa cha bonde tajiri

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Jeshi la adui litaponda walevi wenye kiburi wa Samaria kana kwamba walikuwa wakiponda maua chini ya miguu yao"

litakuwa kama mtini ulioiva ... hugugumia chini

Hii inazungumzia wanajeshi wa adui kuona uzuri wa Samaria na kupora kwa haraka kana kwamba walikuwa mtu ambaye huona mtini wa kwanza wa msimu na kula haraka.

Isaiah 28:5

Yahwe wa majeshi

Yahwe wa majeshi ya Israeli.

atakuwa taji zuri na taji lenye uzuri

Yahwe anazungumziwa kana kwamba alitakiwa kuwa taji zuri ambalo watu wanaomheshimu kama mfalme wao wa kweli wangevaa.

taji zuri na taji lenye uzuri

Hii ina maana ya kitu kimoja. "taji zuri"

watu wake, roho ya haki kwa ajili yake ambaye hukaa katika hukumu, na nguvu

Hii inaweza kuandikwa ili kwamba nomino dhahania "haki" inaelezwa kama kitenzi "kuwa na haki". "watu". Yahwe atasababisha waamuzi kuwa na haki na kutoa nguvu"

roho ya haki

Mtu ambaye ana "roho ya haki" ni mtu ambaye ana sifa za haki na ni mtu mwenye haki.

hukaa katika hukumu

Lahaja hii ina maana ya mtu ambaye ana mamlaka ya kuhukumu.

na nguvu kwa wale ambao huwageuza maadui zao katika malango yao

Hapa "kuwageukia" ni lahaja ambayo ina maana ya kushinda vitani. "na Yahwe atasababisha wanajeshi kuwa na nguvu ili kwamba wawashinde adui zao pale ambapo maadui wanashambulia mji wao"

Isaiah 28:7

Lakini hata hawa

"Lakini hata viongozi"

Kuhani na nabii

Hii haimaanishi kuhani mmoja au nabii. Ina maana ya makuhani na manabii kwa ujumla. "Makuhani na manabii"

hupepesuka kwa mvinyo, na kuyumbayumba kwa kinywaji kikali

Misemo hii miwili ina maana moja na inasisitiza ya kwamba makuhani na manabii hawawezi kufanya kazi yao kwa sababu wamelewa sana. "kujikwaa kwa sababu wamelewa"

wanamezwa kwa mvinyo

Kunywa kwao sana hadi wanashindwa kufikiri kwa usahihi inzungumziwa kana kwamba mvinyo imewameza. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "divai inawafanya kuchanganyikiwa"

wayumbayumba katika kuangalia na kupepesuka katika maamuzi

Kama ambavyo wamelewa sana kutembea sawa sawa, wamelewa sana kuelewa maono Mungu anayowapatia au kufanya maamuzi sahihi.

Isaiah 28:9

Ni kwa nani atamfundisha maarifa, na kwa nani ataelezea ujumbe?

Manabii na makuhani walevi wanatumia swali kumkosoa Isaya, ambaye anajaribu kuwasahisha. "Manabii walevi na makuhani wanasema, 'Isaya hatakiwi kujaribu kutufundisha kuhusu ujumbe wa Yahwe!'"

Kwa wale ambao wameachishwa maziwa au kwa wale ambao wameondolewa tu kutoka kwenye titi?

Manabii na makuhani walevi wanatumia swali kumkosoa Isaya, kwa sababu wanahisi ya kwamba anawafanya kama watoto. "Hatakiwi kutufanya kama watoto!"

Kwa maana ni amri baada ya amri, amri juu ya amri; utawala juu ya utawala, utawala juu ya utawala; hapa kidogo, pale kidogo

Manabii na makuhani walevi wanamkosoa Isaya kwa sababu wanahisi Isaya anarudia amri za kawaida kana kwamba alikuwa akiongea kwa mtoto.

Isaiah 28:11

kwa midomo ya kukejeli na ulimi wa kigeni atazungumza kwa watu hawa

Hapa "midomo" na "ulimi" inawakilisha wageni ambao huongea lugha tofauti na wanayozungumza Waisraeli. Inadokezwa ya kwamba hii ina maana ya jeshi la Ashuru ambalo litashambulia Israeli. "Yahwe atazungumza kwa watu hawa kupitia majeshi ya maadui ambao wataongea lugha ya kigeni"

midomo ya kukejeli

"midomo yenye kigugumizi"

Haya ni mapumziko

Nomino dhahania "pumziko" inaweza kuandikwa kama kivumishi. "Hii ni sehemu ya kupumzika"

toa mapumziko kwake ambaye amechoka

Nomino dhahania "pumziko" inaweza kuwekwa kama kitenzi. "acha yule ambaye amechoka aje na apumzike"

hiki ni kiburudisho

Nomino dhahania "kiburudisho" inaweza kuwekwa kama kitenzi. "hii ni seheu ambayo unaweza kuburudika"

Isaiah 28:13

Kwa hiyo neno la Yahwe

Hapa "neno" linawakilisha ujumbe. "Kwa hiyo ujumbe wa Yahwe"

amri juu ya amri, amri juu ya amri; utawala juu ya utawala, utawala juu ya utawala; hapa kidogo, pale kidogo

Haya ni maneno ambayo makuhani na manabii walevi walitumia jinsi Isaya anawafundisha wao.

ili kwamba waweze kuondoka na kuanguka nyuma, na kuvunjika, kutegwa na kukamatwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "ili kwamba jeshi la Ashuru litakuja na kuwashinda na kuwachukua kama mateka"

kuondoka na kuanguka nyuma

Watu kushindwa vitani kwa jeshi la adui linazungumziwa kana kwamba watu wataanguka chini na kuvunjika.

kutegwa

Wanajeshi wa adui kukamata watu wa Israeli inazungumziwa kana kwamba walikuwa wawindaji ambao hushika mnyama katika mtego.

Isaiah 28:14

Kwa hiyo sikiliza neno la Yahwe

Isaya sasa anazungumza kwa viongozi wa Yerusalemu. Hapa "neno" linawakilisha ujumbe. "Kwa hiyo sikiliza kwa ujumbe wa Yahwe"

Tumefanya agano na kifo, na kwa kuzimu tumefikia makubaliano

Kauli hizi mbili zina maana moja. Maana zinaweza kuwa 1) viongozi wa Yerusalemu wametumia mazingaombwe au uchawi kujaribu kufanya makubaliano na miungu ya sehemu za wafu ili kwamba miungu hawa wawalinde kutokufa au 2) hii ni sitiari ambayo inazungumzia viongozi kufanya makubaliano na viongozi wa Misri. Viongozi wa Yerusalemu walikuwa wanajiamini sana hadi Wamisri wangewalinda na kuonekana kana kwamba walifanya makubaliano na miungu wa sehemu ya wafu.

Kwa hiyo mjeledi mkubwa kabisa utakapopita katikati, hautatufikia sisi

Hii inazungumzia hukumu ya Yahwe na adhabu kana kwamba ilikuwa mjeledi ambao ungewapiga watu. Na mjeledi unazungumziwa kana kwamba ulikuwa mafuriko ambayo yangepita katikati ya Yerusalemu. "Kama matokeo, ambapo wengine wote wanateseka na kufa, hakuna kitu kitatudhuru"

Kwa kuwa tumetengeneza uongo kimbilio letu, na kujiweka hifadhi katika uongo

Misemo hii miwili ina maana moja. "Uongo" unazungumziwa kana kwamba ilikuwa sehemu ambayo mtu angeweza kwenda kujificha. Viongozi wa Yerusalemu wasingesema wanatumaini katika uongo. Waliamin walikuwa salama kabisa. Lakini Isaya anajua hawako salama, kwa sababu wanaamini katika uongo. "Kwa maana uongo umekuwa kama sehemu ambayo tunaweza kujificha kutoka hatarini"

uongo kimbilio letu ... kujiweka hifadhi katika uongo

Maana zaweza kuwa 1) viongozi wanaamini katika uongo ambao wamesema ili kujilinda wenyewe au 2) viongozi huamini ya kwamba agano walilofanya na miungu ya uongo ya sehemu ya wafu itawaweka salama au 3) viongozi huamini ya kwamba makubaliano ambayo wameyafanya na Wamisri itawaweka salama.

Isaiah 28:16

Tazama

"Sikiliza hili"

Nitatandaza Sayuni jiwe la msingi ... msingi wa hakika

Yahwe kumtuma mtu mwenye nguvu kusaidia watu wa Israeli inazungumziwa kana kwamba Yahwe anajenga msingi wa nguvu kwa ajili ya jengo.

jiwe lililojaribiwa

"jiwe ambalo ni thabiti"

msingi wa hakika

"mhimili imara"

Yule ambaye huamini hataaibika

"Yeyote ambaye huamini katika jiwe hili la msingi hatajilaumu"

Isaiah 28:17

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kulinganisha kile atakachofanya kwa ajili ya watu wa Yerusalemu kwa mjenzi kuandaa jengo.

Nitafanya hukumu fimbo ya kupimia, na haki timazi

Yahwe kujaribu kulingana na hukumu yake na haki kuthiibitisha kama watu wana haki inazungumziwa kana kwamba alikuwa mjenzi akitumia vifaa kuthibitisha ya kwamba kitu ni urefu sahihi na usawa wa kamili.

fimbo ya kupimia

Mjenzi hutumia fimbo ya kupimia kubainisha kama kitu kina urefu sahihi.

timazi

Mjenzi hutumia fimbo ya kupimia kubainisha kama kitu kipo wima na usawa.

Mvua ya mawe itaondoa

Yahwe kusababisha kiasi kikubwa cha mvua ya mawe kuanguka inazungumziwa kana kwamba itakuwa mafuriko makubwa. "Mvua za mawe zitaangamiza"

Mvua ya mawe ... maji ya mafuriko

Maana zaweza kuwa 1) maneno yenye maana sawa yanayowakilisha kitu chochote kwa ujumla ambacho kitasababisha uharibifu au 2) hizi ni sitiari kwa jeshi la adui ambalo Yahwe atalituma kuangamiza watu wa Yerusalemu.

Mvua ya mawe

Vipande vikubwa vigumu vya barafu ambavyo huanguka kutoka angani

kimbilio la uongo ... sehemu ya kujificha

Hii inazungumzia kuhusu "uongo" kana kwamba ulikuwa sehemu ambao mtu angeweza kwenda kujificha. Inawakilisha kile viongozi wa Yerusalemu waliamini kuwaweka salama kwa adhabu ya Yahwe. Maana zaweza kuwa 1) viongozi wanaamini katika uongo wao wenyewe ambao wamesema ili kujilinda wenyewe au 2) viongozi wanaamini ya kwamba agano walilofanya na miungu ya uongo ya sehemu ya wafu itawaweka salama au 3) viongozi wanaamini ya kwamba makubaliano na Wamisri yatawaweka salama.

Isaiah 28:18

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Yerusalemu.

Agano lako na kifo litayeyushwa, na makubaliano yako na kuzimu hayatasimama

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Nitafuta agano ambalo umefanya na kifo, na nitafuta makubaliano uliyofanya na kuzimu"

agano lako na kifo ... makubaliano na kuzimu

Maana zaweza kuwa 1) viongozi wa Yerusalemu wametumia mazingaombwe au uchawi kujaribu kufanya makubaliano na miungu ya sehemu za wafu ili kwamba miungu hawa wawalinde kutokufa au 2) hii ni sitiari ambayo inazungumzia viongozi kufanya makubaliano na viongozi wa Misri. Viongozi wa Yerusalemu walikuwa wanajiamini sana hadi Wamisri wangewalinda na kuonekana kana kwamba walifanya makubaliano na miungu wa sehemu ya wafu.

hayatasimama

"hayatadumu"

Pale ambapo mafuriko makali yatakapopita

Maana zaweza kuwa 1) "mafuriko" ni maneno yenye maana sawa na yanawakilisha kitu chochote kwa ujumla ambacho kitasababisha uharibifu au 2) "mafuriko" ni sitiari inayomaanisha jeshi la adui ambalo Yahwe atatuma kuangamiza watu wa Yerusalemu.

utazidiwa nayo

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "itakuzidia" au "itakuangamiza"

asubuhi kwa asubuhi

Hii ni lahaja. "kila siku"

kwa mchana na usiku

Hii ina maana "katika siku nzima"

Isaiah 28:20

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Yerusalemu.

Kwa maana kitanda ni kifupi sana kwa mtu kujinyosha juu, na blangeti ni nyembamba sana kwake kujifunika ndani yake

Huenda hii ilikuwa methali ambayo watu walijua katika kipindi hicho. Ina maana ya kwamba kile wanachoamini kitawaweka salama kutoka kwa adhabu Yahwe atawaangusha kama kitanda ambacho ni kifupi mno au blangeti ambayo ni nyembamba mno.

Yahwe atainuka

Yahwe kujiandaa kutenda inazungumziwa kana kwamba alikuwa amekaa na kisha kuinuka.

Mlima Perasimu ... Bonde la Gibeoni

Hii ina maana ya sehemu ambazo Mungu aliwashinda kwa miujiza majeshi ya adui.

atajiamsha yeye

"atakuwa na hasira sana"

kazi yake ya ajabu ... tendo lake la ajabu

Misemo hii miwili ina maana moja. Kazi hii ni ya ajabu kwa sababu Mungu anatumia jeshi geni kuwashinda watu wa Yerusalemu kuliko kusaidia watu wa Yerusalemu kushinda adui zao.

Isaiah 28:22

Sasa

Hii haimaanishi "katika kipindi hiki", lakini inatumika kuvuta nadhari kwa lengo muhimu ambalo linafuata.

vifungo vyako vitakazwa

Yahwe kuadhibu watu kwa ukali zaidi inazungumziwa kana kwamba angekaza vifungo vyao. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe atakaza vifungo vyako" au "Yahwe atakuadhibu kwa ukali zaidi"

Yahwe wa majeshi

Yahwe wa majeshi ya Israeli.

maagizo ya uharibifu katika dunia

Hii inaweza kuandikwa ili kwamba nomino dhahania "uharibifu" uelezwe kama kitenzi "angamiza". "ya kwamba anakwenda kuangamiza watu katika nchi"

Isaiah 28:23

Taarifa ya Jumla

Hii inaanza mfano ambao unaisha katika 28:29

Zingatia kwa makini na sikilizia sauti yangu; uwe msikivu na sikiliza maneno yangu

Misemo hii miwili ina maana moja. Msemo wa pili unatumka kuimarisha wa kwanza.

sauti yangu

Hapa "sauti" inawakiliisha kile Isaya anasema. "kwa kile nachosema"

maneno yangu

Hapa "maneno" yanawakilisha ujumbe. "kwa ujumbe wangu"

Je! mkulima anayelima siku nzima kupanda, huwa analima tu? Je! huwa anaendelea kuvunja na kupiga haro shamba?

Isaya anatumia maswalii ya balagha kufanya watu wafikiri kwa undani. "Mkulima halimi ardhi tena na tena na kuendelea kufanya kazi bila kupanda mbegu"

Isaiah 28:25

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kuwaambia mfano watu wa Yerusalemu.

Atakapokuwa ameandaa ardhi

"Mkulima alipolima udongo"

je! hatawanyi mbegu ya kisibiti, kupanda jira, kuweka ngano katika mistari na shayiri katika sehemu sahihi, na kusemethi katika mipaka yake?

Isaya anatumia swali kuwafanya watu wa Yerusalemu kuwaza kwa ndani. "hakika atapanda kila aina ya mbegu kwa njia sahihi katika seheu sahihi".

kisibiti ... jira

Haya ni majina ya mimea ambayo ni viungo.

ngano ... shayiri ... kusemethi

Haya ni majina ya mimea ambayo ni nafaka.

Mungu wake humwelekeza; humfundisha kw hekima

Misemo hii miwili ina maana moja. "Yahwe humsaidia mkulima kujua namna ya kutunza kila aina ya mmea"

Isaiah 28:27

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kuwaambia mfano watu wa Yerusalemu.

mbegu ya kisibiti haipurwi kwa nyundo ya kupura

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "mkulima hagawanyish mbegu ya kisibiti kutoka kwa mmea kwa rungu nzito"

kisibiti

Haya ni majina ya mimea ambayo ni viungo.

wala gurudumu la gari huviringishwa juu ya jira

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "wala waviringisha gurudumu ziito juu ya mbegu ya jira"

jira

Haya ni majina ya mimea ambayo ni viungo.

lakini kisibiti inapigwa kwa kijiti, na jira kwa rungu

Isaya anafafanua njia sahihi ya mkulima kutenganisha mbegu kutoka kwa mmea. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "lakini hupiga kisibti kwa fimbo, na hupiga jira kwa rungu"

Nafaka ni ardhi kwa mkate lakini sio kwa ubora sana

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Mkulima husaga nafaka kwa ajili ya mkate lakini sio kwamba iwe ndogo sana"

Isaiah 28:29

Hii pia huja ... bora katika hekima

Hii inahitimisha mfano ulioanza katika 28:23. Somo linalodokezwa la mfano ni kwamba wakulima wana hekima ya kutosha kusikiliza maagizo ya Yahwe kuhusu kupanda na kupura. Lakini viongozi wa Yerusalemu ni wapumbavu kwa kutosikia maagizo ya Yahwe ya kwamba anazungumza kupitia Isaya.

Yahwe wa majeshi

Yahwe wa majeshi wa Israeli.

Isaiah 29

Isaiah 29:1

Ole wa Arieli

Hapa "Arieli" inawakilisha watu ambao wanaishi katika mji wa Arieli. "Jinsi gani itakuwa vibaya kwa watu wa Arieli"

Arieli

Hili ni jina lingine kwa ajili ya Yerusalemu, na lina maana ya "madhabahu".

Daudi alipoweka kambi

"Daudi alikaa" au "Daudi aliishi"

Ongeza mwaka kwa mwaka; acha sikukuu ziwadie

"endelea kusherehekea sikukuu yako mwaka baada ya mwaka". Hili ni tamko la kejeli. Yahwe anawaambia watu kuendelea kusherehekea sikukuu zao ambapo wanatoa sadaka kwake, lakini anajua haitamzuia kuwaangamiza.

Lakini nitazingira

Neno "nitazingira" ina maana ya Yahwe. Hii inawakilisha Yahwe kusababisha jeshi la adui kuzingira Yerusalemu.

atakuwa

Hapa "atakuwa" ina maana ya Arieli, ambayo inawakilisha watu wa Arieli. "watu wa Arieli wata"

kulia na kuomboleza

Maneno "kulia" na "kuomboleza" ina maana moja na inasisitiza ukali wa maombolezo. "wataomboleza kwa uchungu"

kama Arieli

Jina la Arieli lina maana ya "madhabahu"

Isaiah 29:3

Nitapiga kambi dhidi yako

Neno "nitapiga" ina maana ya Yahwe. Hii inawakilisha Yahwe kusababisha jeshi la adui kuziingira Yerusalemu. "Nitaamuru jeshi la adui zako kukuzingira"

uzio ... kazi za kuzingira

"Uzio" ni mnara ambao majeshi hujenga kushambulia miji kwa kuta ndefu. Pia, "kazi za kuzingira" ina maana ya silaha za aina nyingine majeshi hujenga kushambulia miji.

Utawekwa chini

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Adui wako atakuleta chini" au "Adui wako atakushusha"

na utazungumza kutoka ardhini; usemi wako utakuwa chini kutoka mavumbini. Sauti yako itakuwa kama zimwi kutoka kwenye ardhi, na usemi wako utakuwa dhaifu sana kutoka mavumbini

Kauli hizi zote zina maana moja. Zinasisitiza ya kwamba watu ambao hapo awali walizungumza maneno ya kujivuna watakuwa dhaifu na kulia baada ya adui kuwashinda. "na utaweza tu kuonge kwa minong'ono dhaifu kama ya roho inayozungumza ambapo wafu huishi"

Isaiah 29:5

Umati wa wavamizi wako watakuwa kama vumbi dogo, na wingi wa walio wakatili kama makapi ya majani ambacho hupita mbali

Hii inasisitiza jinsi jeshi linalovamia ni dhaifu na lisilo na maana mbele za Mungu. "Yahwe ataondoa kirahisi umati wa wavamizi wako na wingi wa walio katili"

umati wa mavazi yako

"wanajeshi wengi watakushambulia"

walio wakatili kama makapi ya majani

"wanajeshi ambao hawataonyesha huruma watakuwa kama makapi ya majani"

Yahwe wa majeshi atakuja kwako

Neno "kwako" ina maana ya watu wa Yerusalemu. Maana zaweza kuwa 1) "Yahwe wa majeshi atakuja kukusaidia" au 2) "Yahwe wa majeshi atakuja kukuadhibu"

Isaiah 29:7

Itakuwa kama ndoto, maono ya usiku

Msemo "maono ya usiku" ni jambo sawa na "ndoto". Misemo hii inasisitiza ya kwamba hivi karibuni itakuwa kama jeshi linalovamia halikuwa pale.

Umati wa mataifa yote

"Majeshi makubwa kutoka mataifa yote"

watapigana dhidi ya Arieli

Jina "Arieli" ni jina lingine kwa Yerusalemu, na inawakilisha watu ambao wanaishi kule. "kupigana dhidi ya watu wa Arieli"

ngome yake. Watamshambulia na kuimarishwa kwake kugandamiza juu yake

Neno "yake" ina maana ya Arieli ambayo inawakilisha watu ambao wanaishi kule. "ngome zao. Watashambulia mji wa Arieli na ulinzi wake na kusababisha watu kuwa katika mateso makubwa"

itakuwa kama vile mtu mwenye njaa anavyoota anakula ... kiu yake haikatwi

Tashbihi ina maana ya kwamba adui atategemea ushindi lakini watashindwa kwa sababu Mungu hataruhusu wao kushinda Yerusalemu.

Ndio, ndivyo itakavyokuwa idadi kubwa ya mataifa ambayo hupigana dhidi ya Mlima Sayuni

Hapa "Mlima Sayuni" inawakilisha watu ambao wanaishi kule. "Ndio, hivi ndivyo itakavyotokea kwa majeshi kutoka kwa mataifa ambayo hupigana dhidi ya watu wanaoishi juu ya Mlma Sayuni"

Isaiah 29:9

Jishangaze mwenyewe na ushangazwe

Neno "mwenyewe" lina maana ya watu wa Yerusalemu. Kwa nini wanashangazwa inawvza kuwekwa wazi. "Ushangazwe kwa kile nachotaka kukuambia"

jipofushe na uwe kipofu

Watu kupuuza kile Yahwe anasema inazungumziwa kana kwamba wangeweza kujifanya vipofu wenyewe. "endelea kuwa mjinga na kipofu wa kiroho kwa kile nachokuonyesha"

Lewa, lakini sio kwa divai; pepesuka, lakini sio kwa mvinyo

Watu kutokuwa na ufahamu na kutoelewa kile Yahwe anafanya inazungumziwa kana kwamba walikuwa wamelewa. "Uwe bila ufahamu kama mtu mlevi, lakini sio kwa sababu umekunywa divai au mvinyo kupitiliza"

Kwa maana Yahwe amekumwagia juu yako roho ya usingizi mzito

Hapa " roho ya" ina maana "kuwa na sifa za" kuwa na usingizi. Yahwe kusababisha watu kuwa na usingizii inazungumziwa kana kwamba "roho" ilikuwa kimiminiko ambacho kilimwagwa juu ya watu. Pia "usingizi mzito" ni sitiari ambayo ina maana ya watu ambao hawana ufahamu na hawawezi kuelewa kile Yahwe anafanya. "Sababu hauna ufahamu ni kwa sababu Yahwe amesababisha uwe umelala kiroho"

Ameyafumba macho yako, manabii, na amefunika vichwa vyako, watazamaji

Yahwe kusababisha watu kutokuwa na ufahamu na kutoelewa kile anachofanya inazungumziwa kana kwamba alifumba macho yao na kufunika vichwa vyao ili wasiweze kuona. "Ni kana kwamba Yahwe amefumba macho ya manabii na kufunika vichwa vya watazamaji"

Isaiah 29:11

Ufunuo wote umekuwa kwako kama maneno ya kitabu kilichofungwa kabisa

Nabii mwingine Yerusalemu hawawezi kusikia au kuelewa ujumbe wa Mungu. "Yote ambayo Yahwe amefunua kwako ni kama kitabu kilichofungwa kabisa"

kilichofungwa, ambacho watu wanaweza kutoa kwa yule ambayo amesoma

Hii inaweza kuandikwa kama sentensi mpya. "inafungwa kabisa. Mtu anaweza kuchukua kitabu kilichofungwa kabisa kwa mtu ambaye anaweza kusoma"

kama kitabu kinatolewa kwa yule ambaye hawezi kusoma

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Kama mtu anachukua kitabu kwa mtu ambaye hawezi kusoma"

Isaiah 29:13

Watu hawa huja karibu na mimi kwa vinywa vyao na kuniinua mimi kwa midomo yao

Maneno "vinywa" na "midomo" inawakilisha kile watu wanasema. Hapa pia inawakilisha kusema kitu lakini sio kukimaanisha kihalisia. "Watu wa Yerusalemu wanavunga kuniabudu na kuniheshimu kwa kile wanachosema"

lakini moyo wao upo mbali na mimi

Hapa "moyo" ni neno linalowakilisha mawazo ya mtu na hisia. Watu kutokuwa na kujizatiti kwa Yahwe inazungumziwa kana kwamba mioyo yao ilikuwa mbali sana kutoka kwake. "lakini hawaniheshimu katika mawazo yao" au "lakini hawajizatiti kwangu kiukweli"

Heshima yao kwangu ni amri to ya watu ambayo imefundishwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Wananiheshimu tu kwa sababu hicho ndicho watu wanawaambia kufanya"

Kwa hiyo, tazama, nitaendelea kufanya jambo la ajabu katika hawa watu, ajabu baada ya ajabu

"Kwa hiyo, tazama na angalia! ninaenda kufanya mambo mazuri na ya ajabu miongoni mwako ambayo hutaweza kuyaelezea"

Hekima ya watu wenye hekima wao itatoweka, na uelewa wa watu wenye busara wao itapotea

Kauli hizi mbili zina maana moja. Yahwe kuonyesha ya kwamba watu wenye hekima hawawezi kuelewa au kufafanua kile Yahwe anafanya inazungumziwa kana kwamba hekima yao na uelewa utapotea.

Isaiah 29:15

Taarifa ya Jumla

Huyu anaweza kuwa Isaya akizungumza au inaweza kuwa muendelezo wa maneno ya Yahwe katika 29:13-14.

ambao huficha kwa chini kabisa mipango yao kutoka kwa Yahwe

Watu kujaribu kutengeneza mipango bila Yahwe kujua inazungumziwa kana kwamba kama wanaficha mipango yao katika sehemu ya chini ambapo Yahwe hawezi kuona. "ambao wanajaribu kumzuia Yahwe kutogundua kile wanachopanga kufanya"

ambao mateno yao yamo gizani

Inadokezwa ya kwamba wanafanya mambo maovu kwa siri. "ambao hufanya mambo maovu gizani ili mtu asiwaone"

Ambao hutuona, na ambao wanatujua sisi?

Wanatumia swali kusisitiza ya kwamba wanaamini hakuna mtu anayejua kile wanachofanya. "Hakuna mtu, hata Yahwe, anatuona au kujua kile tunachofanya!"

Isaiah 29:16

Unageuza vitu juu chini

Hii ni lahaja ambayo ina maana ya kupotosha kile kilicho cha ukweli. "Unafanya vitu kinyume na namna vinavyotakiwa kuwa" au "Unatakiwa kupotosha ukweli"

Je! mfinyanzi achukuliwe kama udongo, ili kwamba kitu ambacho kimetengenezwa kiweze kusema juu yake ambaye amekitengeneza ... "Yeye haelewi"?

Yahwe ambaye aliumba wanadamu inazungumziwa kana kwamba alikuwa mfinyanzi na wanadamu walikuwa udongo. Sitiari hi nasisitiza ya kwamba ni upumbavu kwa wanaamu kukataa au kukosoa yule ambaye aliviumba. "Je! utanichukulia, muumba wako, kuwa kama udongo badala ya mfinyanzi? Ni kana kwamba mfinyanzi aliumba kitu, na hicho kitu kikasema kuhusu mfinyanzi, "Hakuniiumba mimi", au "Haelewi"

e! mfinyanzi achukuliwe kama udongo ... "Yeye haelewi'"?

Swali hili linatumika kukaripia watu wa Yerusalemu. "Ni dhahiri, mfinyanzi hatakiwi kuchukuliwa kama udongo ... "Yeye haelewi'"

Isaiah 29:17

Lebanoni itageuzwa kuwa shamba, na shamba litakuwa msitu

Maana zaweza kuwa 1) huu ni uhalisi na Yahwe atasababisha maeneo ambapo miti iliota pori katika Lebanoni kuwa mashamba yanayozaa au 2) hii ni sitiari na misitu mikubwa ya Lebanoni inawakilisha wakandamizaji wenye nguvu, na mazao ambayo huota katika shamba na kuwa msitu ni watu wa kawaida ambao wanateseka. Hii ina maana Yahwe atawashusha wale ambao ni wenye nguvu, lakini atawainua wale ambao wanateseka.

Lebanoni itageuzwa kuwa shamba

Hapa "Lebanoni" inawakilisha msitu mkubwa wa mvinje wa Lebanoni. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Mungu atageuza msitu mkubwa wa Lebanoni kuwa shamba"

kiziwi atasikia maneno ya kitabu, na macho ya kipofu yataona giza nene

Maana zaweza kuwa 1) huu ni uhalisi na Yahwe atasabisha watu viziwi kusikia na watu vipofu kuona au 2) hii ni sitiari ya kwamba Yahwe atawezesha watu kusikia na kuelewa ujumbe wake au 3) inaweza kumaanisha zote 1 na 2.

macho ya kipofu

Hapa "macho" yanawakilisha mti kamili. "wale ambao ni vipofu"

Waliokandamizwa watafurahi tena katika Yahwe, na maskini miongoni mwa watu watafurahi katika Mtakatiifu wa Israeli

Misemo hii miwili ina maana moja. "Maskini na watu waliokandamizwa watafurahi tena kwa sababu ya kile Yahwe , Mtakatifu wa Israeli, alichofanya"

Isaiah 29:20

Kwa maana wakatili watakoma

Kivumishi kiidogo "wakatili" kinaweza kuwekwa kama kivumishi. "Kwa maana watu wakatili watakoma" au "Kwa kuwa hapatakuwa tena na watu katili"

na mwenye dharau atatoweka

Kivumishi kidogo "mwenye dharau" kinaweza kuandikwa kama kitenzi. "na wale ambao hudharau watatoweka" au "na watu ambao hukejeli watapotea"

Wote wale ambao hupenda kutenda uovu wataondoshwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe ataondosha wote wale ambao hupenda kutenda uovu"

ambao kwa neno humfanya mtu kuwa mhalifu

Hapa "neno" linawakilisha ushuhuda mahakamani. "ambao husem mahakamani ya kwamba mtu asiye na hatia ana hatia ya kufanya jambo baya"

Wanalaza mtego kwa ajili yake atafutaye haki katika lango na kuiweka haki chini kwa uongo mtupu

Watu waovu kufanya chochote wawezacho kumzuia mtu mwema inazungumzwa kana kwamba watu waovu waliweka mtego kama mwindaji akikamata mawindo. "Wanadanganya na kujaribu kuzuia wale ambao wanataka kufanya kiilicho haki na sahihi"

atafutaye haki katika lango

Malango ya mji mara kwa mara yalikuwa sehemu ambapo viongozi wa mji walifanya maamuzi rasmi.

Isaiah 29:22

nyumba ya Yakobo

Hapa "nyumba" inawakiliisha familia. "vizazi vya Yakobo"

ambao walimkomboa Abrahamu

Hii huenda ina maana ya pale Yahwe alipomwita Abrahamu kutoka katika nchi yake ya nyumbani na kumtuma katika nchi ya ahadi.

Yakobo hata ... uso wake ...atakapowaona watoto wake

Hapa "Yakobo" inawakilisha vizazi vyake. "Vizazi vya Yakobo havitakuwa tena ... nyuso zao ... wataona watoto wao"

wala uso wake kupauka

Hii ni lahaja ambayo ina maana ya hawatakuwa na hofu tena. "wala hawataogopa"

Lakini atakapowaona watoto wake, kazi ya mikono yangu

Hapa "mikono" inawakilisha nguvu na matendo ya Yahwe. "Watakapowaona watoto wote niliowapatia na yote niliyofanya"

watafanya jina langu kuwa takatifu

Hapa "jina" linawakilisha Yahwe. "wataniinua mimi"

Watafanya jina kuwa takatifu la Mtkatifu wa Yakobo

Hapa "jina" linawakilisha Yahwe. Yahwe anajitambua mwenyewe kama "Mtakatifu wa Yakobo". "Wataninua mimi, Mtakatifu wa Yakobo"

wa Mungu wa Israeli

Yahwe anajitambua mwenyewe kama "Mungu wa Israeli". "wa kwangu, Mungu wa Israeli"

Wale wanaopotoka katika roho

Hapa "roho" inawakilisha undani wa mtu. "Wale ambao wamekosea kwa kiile wanachowaza" au "Wale ambao wanakosea katika mtazamo wao"

watapata uelewa

Hii inaweza kufanywa waz zaidi kufafanua kile watakachoelewa. "wataanza kumuelewa Yahwe na sheria zake"

walalamishi watajifunza maarifa

Hii inaweza kuwekwa wazi kufafanua ni maarifa yapi watajifunza. "wale ambao wanalalamika wataanza kujua ya kwamba kile Yahwe anawafundisha ni cha kweli"

Isaiah 30

Isaiah 30:1

watoto waasi

Yahwe anazungumzia kuhusu watu wake kana kwamba walikuwa watoto wake.

hili ni tamko la Yahwe

Hii inaweza kuandikwa ili kwamba nomino dhahania "tamko" inaelezwa kama kitenzi "kusema kwa dhati". "hiki ndicho kile Yahwe anachotamka" au "hiki ndicho kile Yahwe amesema kwa dhati"

Wanafanya mipango, lakini sio kutoka kwangu

Hii inaweza kuandikwa ili kwamba nomino dhahania "mipango" iweze kuandikwa kama kitenzi "kupanga". "Wanapanga kufanya mambo, lakini hawaniulizi nini nachotaka wao kufanya"

lakini hawakuongozwa kwa Roho wangu

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "lakini Roho waangu hakuwaongoza"

wanaongeza dhambi kwa dhambi

Kuendelea kutenda dhamb inazungumziwa kana kwamba dhambi iliikuwa maumbo ambayo yaliweza kupangwa juu ya mengine. "wanaendelea kutenda dhambi zaidi na zaidi"

Wanatafuta ulinzi kutoka kwa Farao

Hii inaweza kuandikwa ili kwamba nomino dhahania "ulinzi" inaelezwa kama kitenzi "linda". "Wanamuuliza Farao kuwalinda"

na kufuata kimbilio katika kifuli cha Misri

Ulinzi wa Misri kutoka kwa jeshi la adui unazungumziwa kana kwamba ulikuwa kivuli ambacho hulinda mtu kutoka na joto linalochoma la jua. "wanawategemea Wamisri kuwaweka salama"

Isaiah 30:3

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Yuda.

Kwa hiyo ulinzi wa Farao utakuwa aibu yako, na kimbilio katika kivuli cha Misri, fedheha yako

Hii inaweza kuandikwa ili kwamba nomino dhahania "ulinzi", "aibu", na "fedheha" zinaelezwa kama vivumishi au vitenzi. "Kwa hiiyo utaibika kwa sabbu ulimtegemea Farao kukulinda; utafedheheshwa kwa sababu uliwategemea Wamisri kukuweka salama"

kimbilio katika kivuli cha Misri

Ulinzi wa Misri kutoka kwa jeshi la adui inazungumziwa kana kwamba ulikuwa kivuli ambacho humlinda mtu kutoka na joto linalowaka la jua.

wakuu

Hapa "wakuu" ina maana ya afisa au balozi, sio lazima wana wa mfalme.

wao ... wata ... wao

Maneno haya yana maana ya watu wa Yuda.

Soani ... Hanesi

Hii ilikuwa miji katika sehemu ya kaskazini ya Misri.

wamekuja Hanesi

Hapa "kuja" inaweza kuandikwa kama "kuondoka"

kwa sababu ya watu

"kwa sababu ya watu wa Misri"

Isaiah 30:6

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza tamko la Mungu kuhusu watu wa Yuda.

tamko

"Hiki ndicho Yahwe anachotamka"

ya simba jike na simba, kipiribao na nyoka mkali anayepaa

Hii ina maana ya aina hawa ya wanyama kwa ujumla. "ambapo simba jike na simba huishi, na ambapo kuna kipiribao na nyoka"

nyoka mkali anayepaa

Hapa neno "mkali" huenda una maana ya sumu ya nyoka anapouma na neno "kupaa" lina maana ya kusogea kwake kwa haraka.

wanabeba utajiri wao

"watu wa Yuda wanabeba utajiri wao"

nimemuita Rahabu, ambaye hukaa kwa kutulia

Kulikuwa na simulizi maarufu kuhusu joka la baharini linaloitwa Rahabu. Jina Rahabu ina maana ya "nguvu" au "kiburi". "Ninaita Misri mwenye kiburi wa sauti ambaye hafanyi lolote"

Isaiah 30:8

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na Isaya.

Sasa

Neno hili linatumika hapa kuweka alama ya pumziko katika tamko la Yahwe kuhusu Yuda. Hapa anamwambia Isaya kufanya kitu.

katika uwepo wao

"katika uwepo wa watu wa Yuda"

kwa maana muda umefika

Hii inazungumzia kipindi kana kwamba kinasafiri na kufika mahali. "kwa kipindi cha siku za usoni"

watoto waongo, watoto ambao hawasikii maelekezo ya Yahwe

Hii inazungumzia watu wa Yahwe kana kwamba walikuwa watoto wake. Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi. "Wanaenenda kama watoto ambao hudanganya na kutosikiliza kile Yahwe anachoamuru"

Isaiah 30:10

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza kuhusu watu wa Yuda.

Geuka upande kutoka katika njia, potea kutoka katika njia

Jinsi Yahwe anavyotaka watu wake kuenenda inazungumziwa kana kwamba ilikuwa njia au barabara ambayo inatembelewa. Kutomtii Yahwe inazungumziwa kana kwamba mtu hupotea kutoka katika njia ya Yahwe.

Mtakatifu wa Israeli

Mtakatifu wa Israeli

Isaiah 30:12

Mtakatifu wa Israeli

Mtakatifu wa Israeli

unakataa neno hili

Hapa "neno" inawakilisha ujumbe. "unakataa ujumbe huu"

kuamini katika ukandamizaji na udanganyifu na kuiegemea

Maana zaweza kuwa 1) viongozi wa Yuda wanaamini katika viongozi wa Misri mbao hutawala kwa kukandamiza na kudanganya wengine au 2) viongozi wa Yuda wamekandamiza na kudanganya watu wao wenyewe ili kuchukua fedha zao na kuituma kwa viongozi wa Misri kama malipo kwa ajili ya ulinzi.

kuiegemea

Hapa neno "kuiegemea" ina maana ya "ukandamizaji na udanganyifu". "kuziegemea"

egemea katika

Hii ni lahaja ambayo ina maana ya kuamini au kutegemea juu ya kitu.

kwa hiyo dhambi hii kwako itakuwa kama sehemu iliyovunjika ... kwa mara moja

Tashbihi hii ina maana ya kwamba Mungu ataangamiza watu wa Yuda ghafla kwa sababu ya dhambi zao.

kama sehemu iliyovunjka tayari kudondoka

Inaeleweka ya kwamba hii ni sehemu iliyovunjika ya ukuta. "kama sehemu iliyovunjika ya ukuta ambayo iko tayari kuanguka"

ambao anguko lake litatokea ghafla

Hii inaweza kundikwa ili kwamba nomino dhahania "anguka" inaelezwa kama kitenzi "anguka". "ambayo itaanguka ghafla"

ghafla, kwa mara moja

Hizi zina maana ya kitu kimoja na husisitiza jinsi ukuta utakavyoanguka kwa haraka.

Isaiah 30:14

Taarifa ya Jumla

Isaya anafafanua jinsi Yahwe ataangamiza watu wa Yuda.

Ativunja

Hapa "ataivunja" ina maana ya sehemu ya ukuta ambayo inakaribia kuanguka. Sehemu katika ukuta ni sitiari ambayo inawakilisha watu wa Yuda na dhambi yao iliyotajwa katika 30:12

kama chombo cha mfinyanzi kinavyovunjwa

Tashbihi hii ina maana ya kwamba kipande cha ukuta kitavunjika haraka na kikamilifu kama jagi la udongo linapoanguka chini.

mfinyanzi

Mfinyanzi ni mtu ambaye hutengeneza vyungu na majagi kwa udongo.

hakutapatikana

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "hakuna mtu ataweza kupata" au "hapatakuwa"

kigae ambacho kitatumika kukwangua

"kigae kikubwa ya kutosha kukwangua"

moto kutoka katika meko

Neno "moto" hapa lina maana ya majivu. "majivu kutoka katika sehemu ya moto"

Isaiah 30:15

Mtakatifu wa Israeli

Mtakatifu wa Israeli

Katika kurudi na kupumzika utaokolewa

Kutubu inazungumziwa kana kwamba ilikuwa kurudi kwa Yahwe kihalisia. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Nitakuokoa kutok kwa adui zako kama utatubu na kupumzika ukijua ya kwamba nitakutunza"

kupumzika

Inadokezwa ya kwamba watu hupumzika kwa sababu wanamwaminii Yahwe kuwatunza.

katika utulivu na katika imani itakuwa nguvu yako

Utulivu hapa ina maana ya kutokuwa na wasiwasi. Inadokezwa ya kwamba hawana wasiwasi kwa sababu wanamwamini Yahwe. "Utakuwa na nguvu kama utakuwa kimya na kuniamini mimi"

tutatoroka juu ya farasi

Ni wazi kwamba farasi hizi ndizo ambazo watu wa Yuda walipokea kutoka kwa Wamisri.

Isaiah 30:17

Elfu moja watatoroka katika tishio la mmoja; katika tishio la watano utatoroka

Neno "mwanajeshi" linaeleweka. "Wanajeshi elfu moja watatoroka katika tishio la mwanajeshi mmoja wa adui; katika tishio la wanajeshi watano wa adui wanajeshi wako wote watatoroka"

Elfu moja

"1,000"

mpaka aliyesalia wa kwako ataakuwa kama fimbo ya bendera juu ya mlima, au kama bendera juu ya kilima

Tashbihi hii ina maana ya kwamba kutakuwa na watu wachache sana waliobaki mpaka watakuwa kama bendera moja juu ya kilima.

Isaiah 30:18

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza na watu wa Yuda.

hautalia ... kwako ... atakujibu

Hapa "kwako" ina maana ya watu ambao wanaishi Sayuni.

atakujibu

"atakusaidia"

Isaiah 30:20

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza na watu wa Yuda.

mkate wa shida na maji ya mateso

Hapa "mkate" na "maji" huunda mlo wa mtu maskini sana. Msemo wote unawakilisha nyakati ngumu na umaskini wa watu.

mwalimu wako

Hii ina maana ya Yahwe.

utamwona mwalimu wako kwa macho yako mwenyewe

Hapa "macho" inawakilisha mtu mzima. "nyie wenyewe mtamwona mwalimu wenu"

Masikio yako yatasikia

Hapa "masikio" inawakilsha mtu mzima. "Utasikia"

neno nyuma yako likisema

Hapa "neno" linawakilisha mtu anayezungumza. "yule anayezungumza nyuma yako akisema"

Hii ndiyo njia, tembea juu yake

Jinsi Yahwe anavyotaka watu wake kuenenda inazungumziwa kana kwamba ilikuwa njia au barabara. Kumtii Yahwe inazungumziwa kana kwamba ilikuwa mtu akitembea katika njia yake.

utakapogeuka kulia au utakapogeuka kushoto

Kumkaidi Yahwe inazungumziwa kana kwamb mtu aligeuka kushoto au kulia katika njia ya Yahwe.

Isaiah 30:22

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza na watu wa Yuda.

Utazitupa mbali kama kitambaa cha hedhi

Tashbihi hii ina maana watatupa mbali sanamu zao kana kwamba zilikuwa takataka.

Utasema kwao, "Ondoka hapa"

Hii inazungumzia sanamu kana kwamba zinaweza kusikia na kuinuka na kuondoka mahali. Yahwe ana maana ya kwamba watu hawatahitaji au kutaka tena sanamu.

Isaiah 30:23

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza na watu wa Yuda.

Atatoa

"Yahwe atatoa"

mkate kwa wingi kutoka ardhini

Hapa "mkate" unawakilisha chakula kwa ujumla. "atasababisha ardhi kutoa chakula kingi kwa ajili yako kula"

Katika siku hiyo

Hapa "siku" inawakilisha kipindi cha muda kwa ujumla. "Katika kipindi hicho"

ambayo imepepetwa kwa koleo na uma

Makoleo na uma yalitumika kurusha nafaka angani ili upepo upulize makapi, kuacha tu sehemu ambayo inaweza kuliwa. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "ambayo umepepeta kwa koleo na uma ya nyasi"

Isaiah 30:25

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza na watu wa Yuda.

Katika kila mlima wa juu ... mwanga wa jua wa siku saba

Isaya anafafanua kile itakayokuwa hali sahihi baada ya Yahwe kukomboa watu wake.

katika siku ya machinjo makubwa ambapo minara huanguka

"Yahwe anapochinja adui zako na kusababisha minara yao yenye nguvu kuanguka"

katika siku hiyo

Hapa "siku" inawakilisha kipindi cha muda kwa ujumla. "katika kipindi hicho"

mwanga wa jua utakuwa na mwanga mara saba, kama mwanga wa jua wa siku saba

"jua litang'aa kwa mwanga wa jua saba" au "jua litatoa mwanga mwingi katika siku moja kama linavyotoa katika siku saba"

Yahwe atafunga kuvunjika kwa watu wake na kuponya vilia vya kuwajeruhi kwake

Yahwe kufariji watu wake na kusababisha mateso yao kufika mwisho inazungumziwa kana kwamba angefunga vitambaa juu ya vidonda vyao.

Isaiah 30:27

jina la Yahwe ... kma moto unaoteketeza

Yahwe kuwa na hasira kali inzungumziwa kana kwamba alikuwa moto mkubwa.

jina la Yahwe linakuja

Hapa "jina" linawakilisha Yahwe. "Yahwe anakuja"

Midomo yake imejaa ghadhabu, na ulimi wake ni kama moto unaoteketeza

Hapa "midomo" na "ulimi" ni mifano ya maneno ambayo inawakilisha Yahwe akzungumza. Na, Yahwe anazungumza na hasira kubwa na uwezo ambao unazungumziwa kana kwamba ulimi wake ulikuwa moto. "Anapozungumza hasira yake ni kama moto ambao huangamiza kila kitu"

Pumzi yake ni mbubujiko wa nguvu unaomwagikia

Hii inalinganisha hewa inayotoka mdomoni mwa Yahwe kwa mafuriko kusisitiza nguvu yake ya kuangamiza.

kuchekecha mataifa kwa chungio la uharibifu

Yahwe kutenganisha watu wa mataifa na kuangamiza watu waovu inazungumziwa kana kwamba Yahwe huweka mataifa katika chungio. Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. "Yahwe atatenganisha na kuangamiza watu waovu wa mataifa"

Pumzi yake ni hatamu katika taya wa watu kusababisha wazurure mbali

Yahwe kuwa na nguvu ya kusbabisha mipango ya watu kushindwa au kusababisha waangamizwe inazungumziwa kana kwamba pumzi yake ilikuwa hatamu ambayo huongoza watu nje ya njia sahihi.

hatamu katika taya za watu

"hatamu" ni chombo ambacho watu huwek juu ya kichwa cha farasi kuiongoza. Hatamu huwa na kipande kidogo kinachoitwa "lijamu" ambayo huwekwa katika mdomo wa farasi. "hatamu juu ya vichwa vya watu" au "lijamu katika taya za watu"

Isaiah 30:29

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza na watu wa Yuda.

Utakuwa na wimbo

Hii inaweza kuandikwa ili kwamba nomino dhahania "wimbo" inaelezwa kama kitenzi. "Utaimba"

kama usiku ambapo sikukuu takatifu inazingatiwa

Tashbihi hii inasisitiza jinsi watu watakavyokuwa na furaha.

ambapo sikukuu takatifu inazingatiwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "utakapozingatia sherehe takatifu"

na furaha ya moyo

Hapa "moyo" unawakilisha uanadamu wa ndani wa mtu. "nawe utakuwa na furaha"

kama pale mtu huenda ... Mwamba wa Israeli

Tashbihi hii inasisitiza jinsi watu watakavyokuwa na furaha.

kwa Mwamba wa Israeli

Yahwe kuwa na nguvu ya kulinda watu wake inazungumziwa kana kwamba alikuwa mwamba ambao watu wanaweza kupanda na kutoroka kutoka kwa adui. "kwa mwamba wa ulinzi wa Israeli" au "ambao ni kama mwamba wa ulinzi wa Israeli"

Isaiah 30:30

kuonyesha kusogea kwa mkono wake

Hapa "mkono" unawakilisha nguvu ya Mungu. Inadokezwa ya kwamba Yahwe ataonyesha nguvu yake kwa kuangamiza maadui wa watu wake. "onyesha ya kwamba ana nguvu kwa kuangamiza adui zako"

katika dhoruba ya hasira na miale ya moto

Hasira ya Yahwe inazungumziwa kana kwamba ilikuwa dhoruba au moto. "katika hasira ambayo ni kama dhoruba na miale ya moto" au "katika hasira kuu"

kwa upepo wa dhoruba, mvua ya dhoruba, na mvua ya mawe

"kwa dhoruba iliyojaa upepo, mvua na mvua ya mawe"

mvua ya mawe

vipande vigumu vya barafu ambavyo huanguka kutoka angani kama mvua

Isaiah 30:31

Kwa maana kwa sauti ya Yahwe, Ashuru itapondwapondwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Kwa maana Yahwe anapozungumza atapondaponda wanajeshi wa Ashuru"

Ashuru itapondwapondwa

Isaya anazungumzia hofu ya Ashuru kana kwamba Ashuru ni chombo ambacho sauti ya Yahwe hupondaponda. "Ashuru itaogopa"

Ashuru

Hapa hii inawakilisha wanajeshi wa Ashuru.

Kila pigo la kiboko kilichoteuliwa ambacho Yahwe atakilaza juu yao

Yahwe kusababisha jeshi kuwashinda Ashuru inazungumziwa kana kwamba Yahwe angewapiga Ashuru kwa fimbo.

itaungana

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "watu wa Yuda wataungana nayo"

kigoma

Hiki ni chombo cha muziki chenye kichwa kama ngoma ambacho kinaweza kupigwa na kina vipande vya chuma kuzunguka pande ambazo hutoa sauti pale chombo kinapotikiswa.

anapambana na kupigana pamoja nao

Yahwe kusababisha jeshi la adui kuwashinda Ashuru inazungumziwa kana kwamba Yahwe walikuwa shujaa ambaye angepigana pamoja na jeshi la adui.

Isaiah 30:33

Kwa maana sehemu ya kuchoma iliandaliwa zamani

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Kwa maana zamani Yahwe aliandaa sehemu kwa ajili ya kuchoma"

sehemu ya kuchoma

Msemo huu ni maana ya neno "Tofethi". Tofethi ni sehemu katika Bonde la Hinomi, kusini mwa Yerusalemu, ambapo katika kipindi kimoja watu walichoma watoto wao kama sadaka kwa miungu ya uongo.

inaandaliwaa kwa ajili ya mfalme

Inadokezwa ya kwamba hii ina maana ya mfalme wa Ashuru. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe aliandaa kwa ajili ya mfalme wa Ashuru".

Rundo lipo tayari na moto na mbao nyingi

"Rundo lipo tayari kwa mbao nyingi kutengeneza moto"

Pumzi ya Yahwe, kama kijito cha salfa, kitaiwasha moto

Hii inazungumzia pumzi ya Yahwe kana kwamba ilikuwa mto wa moto ambao utawasha rundo katika moto.

Isaiah 31

Isaiah 31:1

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza kwa watu wa Yuda.

wanaokwenda chini mpaka Misri

Msemo "kwenda chini" inatumika hapa kwa sababu Misri ipo chini kwa kimo kuliko Yerusalemu.

wanaokwenda chini

"watu hao wa Yuda wanaokwenda chini"

kuegemea farasi

Hii inazungumza juu ya watu kutegemea farasi wao kuwasaidia kana kwamba walikuwa wakitegemea farasi wao. "kutegemea farasi wao"

Mtakatifu wa Israeli

"Wameondoka mbali kutoka kwa Yahwe"

wala hawamtafuti Yahwe

"wala hawamuulizi Yahwe kuwasaidia"

ataleta maafa

Hapa neno "ataleta" lina maana ya "kusababisha". "atasababisha maafa kutokea"

hatarudisha maneno yake

Msemo "kurudisha maneno yake" yanazungumzia juu ya mtu kutotimiza kile alichosema atafanya kana kwamba maneno ambayo alisema yalikuwa kitu ambacho angeweza kuvuta kuelekea kwake. Hapa inasema ya kwamba Yahwe hatafanya hivi, ikimaanisha atatekeleza kile alichosema. "atafanya kile alichosema kuwa atafanya"

kuinuka dhidi ya

"kuadhibu"

nyumba ovu

Hii ina maana ya watu waovu wanaoishi pale. "wote wanaofanya mambo maovu"

Isaiah 31:3

Misri ni mwanamume

Hapa Misri ina maana ya wanajeshi wa Misri. "Wanajeshi wa Misri ni wanamume"

farasi wao ni nyama na sio roho

Hii ina maana ya kwamba farasi wao ni farasi tu na sio viumbe vya kiroho. "farasi wao ni farasi tu; sio roho zenye uwezo!"

Yahwe atakapofikia kwa mkono wake

Msemo "mkono" mara kwa mara hutumika kwa kumbukumbu ya matendo na uwezo wa Mungu. "Yahwe hutumia uwezo wake dhidi yao"

wote yule anayesaidia atajikwaa, na yule anayesaidiwa ataanguka

Misemo hii miwili kimsingi ina maana moja. Kujikwaa na kuanguka ni sitiari ya kushindwa. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "vitu hivi viwili vitatokea: nitaiangamiza Misri, inayokusaidia, na nitakuangamiza wewe, ambaye Misri inasaidia"

yule anayesaidiwa ataanguka

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "yule ambaye anatafuta msaada"

Isaiah 31:4

Taarifa ya Jumla

Yahwe anazungumza na Isaya

Kama simba ... ndivyo Yahwe wa majeshi

"Simba ... kwa njia hiyo hiyo Yahwe wa majeshi". Hapa Yahwe anazungumza jinsi atakavyolinda watu ambao ni wake na kutokuogopa kwa kujilinganisha na simba ambaye hulinda mawindo yake"

ndivyo Yahwe wa majeshi atakashuka ... kilima hicho

Inaweza kuwa wazi zaidi kama ukiweka mstari wa mwisho kabla ya mstari wa kwanza. "Yahwe wa majeshi atashuka kupigana juu ya Mlima Sayuni, juu ya mlima huo, kama simba, hata simba mdogo"

simba, hata simba mdogo

"simba jike au simba muuaji". Hii ni jozi ya kufanana ikiwa na misemo miwili kumaanisha simba mkali. "simba"

huunguruma

huonya wengine kukaa mbali

kikundi cha wachungaji kinapoitwa dhidi yake

Msemo huu "kinapoitwa dhidi yake" una maana ya kutumwa kufukuza simba mbali. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "mtu anapowatuma wachungaji kufukuza simba mbali"

kutokana na sauti yao

Wachungaji hutoa sauti za juu kujaribu kufukuza simba mbali. "kutoka kwa sauti za juu ambazo wanazifanya"

atashuka

"watakuja chini". Hii ina maana kushuka kutoka mbinguni. "atakuja chini kutoka mbinguni"

juu ya Mlima Sayuni

Misemo yote miwili ina maana ya Mlima Sayuni. "juu ya Mlima Sayuni"

Isaiah 31:5

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza

Kama ndege wapaavyo, ndivyo Yahwe wa majeshi atalinda Yerusalemu

Hapa njia ambayo Yahwe analinda Yerusalemu inalinganishwa na njia ambayo mama wa ndege hulinda makinda yake katika kiota chao.

atalinda na kuokoa atakapokuwa akipita juu yake na kuitunza

Hii inazungumza jinsi Yahwe anavyolinda na kukoa Yerusalemu, ikimueleza yeye kama ndege ambaye hupaa juu ya mji. "atalinda na kuokoa huo mji kutoka kwa maadui zake"

Yahwe wa majeshi

Hii inaelezea jambo amabalo lingeweza kutokea zamani lakini halikutokea.

Yerusalemu

Hii ina maana ya watu wanaoishi pale. "watu wa Yerusalemu"

Mrudie yeye ambaye ulimuacha kwa kina sana

"Rudi kwa yule ambaye umemuasi"

ambayo mikono yako mwenyewe ilitengeneza kwa dhambi

Hapa watu wanamaanishwa kwa "mikono" yao kusisitiza ya kwamba walitengeneza kitu kwa mikono yao. "ya kwamba umefanya dhambi kwa kutengeneza kwa mikono yako mwenyewe"

Isaiah 32

Isaiah 32:1

Tazama

Neno hili linatumika hapa kuwavuta nadhari ya watu kwa kile kinachosemwa baadaye. "Sikiliza"

Kila mmoja atakuwa kama hifadhi kutoka kwa upepo na kimbilio kutoka kwa dhoruba

Hii inalinganisha mfalme na waku ambao wanalinda watu katika hifadhi. "watawala watalinda watu kama hifadhi inavyofanya katika dhoruba"

kama vijito vya maji katika sehemu kavu

Huu ni ulinganisho mwingine ambao una maana ya watawala kutoa kwa ajili ya mahitaj ya watu. "watatoa kwa ajili ya watu kama vijito vya maji katika sehemu kavu"

kama kivuli cha mwamba mkubwa katika nchi iliyochoka

Huu ni ulinganisho mwingine ambao una maana ya watawala kutoa faraja na pumziko kwa ajili ya watu. "watatoa pumziko kwa ajili ya watu kama mwamba mkubwa unaotoa kivuli kwa watu waliochoka"

Kisha macho ... kwa makini

Misemo hii miwili inasisitiza ya kwamba viongozi watawawezesha watu kuelewa ukweli wa Mungu.

hawatafifia

"wataona vizuri"

Isaiah 32:4

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kufafanua watu baada ya Mungu kuwarejesha watawala wenye haki wa Yuda.

Wenye pupa ... mwenye kigugumizi

Hii ina maana ya watu ambao hufanya kwa pupa na watu wenye kigugumizi. "Mtu mwenye pupa ... mtu mwenye kigugumizi"

Mpumbavu hataitwa tena mwenye heshima

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Hakuna mtu atakayetoa heshima kwa mpumbavu"

Kwa maana mpumbavu huongea upuuzi

"Mpumbavu" ina maana ya watu wapumbavu. Pia, "upuuzi" na "uovu" inaweza kuelezwa kama vivumishi. "Kwa maana mtu mpumbavu anasema vitu vya kipuuzi na moyo wake unapanga mambo maovu"

moyo wake unapanga uovu

Hapa mtu mpumbavu anamaanishwa kwa moyo wake kusisitiza mawazo yake ya ndani. "anapanga mambo maovu moyoni mwake"

wala mdanganyifu hataitwa mwenye msimamo

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Mdanganyifu" ina maana mtu ambaye ni mdanganyifu. "wala hakuna mtu ataonyesha heshima kwa mtu anayedanganya"

Huwafanya

Neno "huwafanya" lina maana ya mtu mpumbavu.

wenye njaa kuwa tupu

"Wenye njaa" ina maana ya watu wenye njaa. Wana njaa kwa sababu wana matumbo tupu. "mtu mwenye njaa ana tumbo tupu"

wenye kiu huwafanya kukosa kinywaji

"Wenye kiu" ina maana ya watu ambao wana kiu. "anasababisha wenye kiu kutokuwa na kitu cha kunywa"

Isaiah 32:7

Mdanganyifu

Hii ina maana ya mtu ambaye hudanganya wengine. "udanganyifu wa mtu"

uharibifu wa maskini kwa uongo

"Maskini" ina maana ya watu maskini. Pia, msemo "kuharibu" haimaanishi kuwaua lakini kuwadhuru kwa kusema uongo juu yao. "kuwadhuru maskini kwa kusema uongo"

atasimama

Hii ina maana ya kwamba atafanikiwa. "atakuwa na mafanikio"

Isaiah 32:9

Inuka

"Simama" au "Zingatia kwa makini"

mliotulia

"salama" au "kuwa huru"

sauti yangu

Isaya ana maana yake mwenyewe kwa sauti yake kusisitiza kiile anachosema. "mimi kuongea"

imani yenu itavunjwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. Pia, Isaya anazungumzia wao kutokuwa na imani kana kwamba imani ilikuwa kitu cha kimwili ambacho kinaweza kuvunjwa. "hautakuwa na imani tena"

mavuno ya zabibu yatashindwa

Hii ina maana ya kwamba hapatakuwa na mizabibu mizuri ya kuvuna. "hapatakuwa na mizabibu kwa ajili yako kuvuna"

makusanyo hayatakuja

"kipindi cha makusanyo ya nafaka hakutatokea"

Isaiah 32:11

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza.

Tetemekeni

"Tetemeka kwa woga"

wametulia

"salama" au "kuwa huru"

vua nguo zako nzuri na jiweke mwenyewe wazi

Hapa "wazi" haimaanishi kuwa uchi, lakini kujifunika kiasi kama vile kwa nguo za ndani. "vua nguo zako nzuri na ujifanye kutokuwa na nguo" au "vua nguo zako za kibunifu"

vaa gunia za nguo kuzunguka viunoni mwako

Hili ni tendo la kulia au kuomboleza. "vaa nguo ya gunia kiunoni unapolia"

Utaomboleza kwa ajili ya mashamba mazuri, kwa ajili ya mizabibu ya matunda

Hii ina maana ya kwamba watalia kwa sauti wanapoomboleza kile knachotokea kwa mashamba yao yaliyozaa na mizabibu. "Utalia kwa sababu ya kile kinachotokea kwa mashamba yako mazuri na mizabibu inayozaa"

miiba na mibigili

Mbigili na miiba mara kwa mara hutumika kama alama za miji na nchi zilizoharibiwa.

nyumba zilizokuwa na furaha mwanzo

Hapa nyumba inafafanuliwa kama kuwa na furaha kwa sababu ya watu wenye furaha ndani mwao. "nyumba zako ambamo mlikuwa na furaha awali"

mji wa furaha

"mji wako wa shangwe". Neno "furaha" ina maana ya kushangilia na kusherekea.

Isaiah 32:14

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza.

Kwa maana kasri litatelekezwa, miji iliyojaa itaachwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Kwa maana watu wataacha kasri na makundi watatelekeza mji"

kilima

Hii ina maana ya ngome iliyojengwa juu ya kilima. "ngome juu ya kilima"

kilima na mnara wa mlinzi vitakuwa mapango

Hii inazungumzia ngoma na mnara kuachwa kana kwamba vimekuwa mapango. "kilima na mnara vitaachwa na kuwa tupu"

furaha ya punda mwitu, malisho ya makundi

Hii ina maana wanyama hawa watafurahiia nyasi ambayo huota miongoni mwa ngome na mnara. "punda mwitu na kundi la kondoo watakula nyasi pale"

milele

Hii ina maana ya muda mrefu sana. "muda mrefu mno"

hadi Roho anapomiminwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "mpaka Yahwe atakapomwaga Roho"

hadi Roho anapomiminwa juu yetu

Hii inazungumzia Yahwe kumpatia Roho kwa watu wake kana kwamba Roho alikuwa mmiminiko ambao unaweza kumwagwa juu yao. "Roho amepatiwa kwetu"

kutoka juu

Hapa mbinguni ina maana ya "juu". "kutoka mbinguni"

mashamba yanayozaa yanachuliwa kama msitu

Hii inaweza kuandikwa katika hali ya kutenda. Hii inalinganisha jinsi mashamba yalivyo na wingi na kuzaa kwa kulinganisha na msitu mnene na mkubwa.

Isaiah 32:16

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza.

hukumu itakaa ... haki itaishi

Isaya anafafanua "hukumu" na "haki" kama mtu ambaye anaishi katika maeneo haya. Hii ina maana ya watu ambao wanaishi katika maeneo haya watafanya kilicho haki na sahihi. "watu watafanya kwa haki katika nyika na watu watatenda kwa haki katika mashamba yenye rutuba.

Kazi ya haki itakuwa amani; na matokeo ya haki, utulivu na imani milele

Misemo hii miwili ni sambamba na yote hutoa matokeo ya haki. Inaweza ikajumlishwa. "Matokeo ya watu kutenda haki ni kwamba kutakuwa na amani, na utulivu na imani milele"

makazi

"sehemu"

Isaiah 32:19

mvua ya mawe

"Mvua ya mawe" hutokea pale ambapo vipande vya barafu huanguka kutoka kwenye anga.

msitu unaangamizwa, na mji unateketezwa kabisa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "inaangamiza msitu na kuangamiza mj kabisa"

wewe ambaye unapanda kando na vijito vyote vitabarikiwa, wewe ambaye unawatuma ng'ombe na punda wako kulisha

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. Hii ina maana ya Yahwe kubariki watu wake wote na inazungumzia vitu ambavyo ni kawaida kwa watu wake kufanya. "Yahwe atakubariki, unapopanda mazao yako katika mashamba kando ya vijito na unatuma ng'ombe wako na punda kulisha katika malisho"

Isaiah 33

Isaiah 33:1

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza kwa shairi kwa ajili ya Yahwe kwa Waashuru.

ambaye haujaangamizwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "ambao wengine hawajawaangamiza"

utaangamizwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "wengine watakuangamiza"

watakusaliti

"wengine watakusaliti"

Isaiah 33:2

kuwa mkono wetu

Hapa mkono wa Yahwe una maana ya nguvu yake. Hii inazungumzia Yahwe kuwaimarisha kana kwamba Yahwe angetumia nguvu yake kutenda kwa ajili yao. "tupatie nguvu"

kila asubuhi

Hii ina maana ya siku nzima, sio asubuhi tu. "kila siku"

wokovu wetu

Neno "wokovu" linaweza kuelezwa kwa kitenzi "okoa". "uwe wokovu wetu" au "tuokoe"

katika kipindi cha shida

Hii in maana ya kipindi ambapo wanapatia shida. "tunapokuwa na shida"

Isaiah 33:3

Kwa sauti kubwa watu wanatoroka

Maana zinazowezekana za "sauti kubwa" ni 1) ina maana ya sauti ya Yahwe. "Watu hutoroka kwa kelele ya sauti yako" au 2) ina maana ya kelele kubwa ya jeshi la Yahwe. "Watu hutoroka kwa sauti ya jeshi lako"

inuka

Hii ina maana kuanza kufanya kitu. "anza kufanya"

mataifa yanatawanywa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "mataifa yanagawanya"

Mali yako iliyoibiwa inakusanywa kama nzige zinavyojikusanya; kama nzige wanavyoruka, watu huruka juu yake

Hii inalinganisha jinsi watu wa Yahwe walivyo na haraka na shauku wanapokusanya mali iliyoibiwa kutoka kwa adui zao. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Watu wako hukusanya mali za kuibiwa kutoka kwa adui zako kwa ukali huo huo kama nzige wanavyomeza mimea ya kijani"

Isaiah 33:5

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumzia watu wa Yuda

Yahwe anainuliwa

"Yahwe ni mkubwa kuliko mtu yeyote yule"

Ataijaza Sayuni kwa hukumu na haki

Hii inazungumzia Yahwe kutawala Sayuni kwa hukumu na haki yake kana kwamba alikuwa akijaza Sayuni kwa hukumu na haki. "Atatawala Sayuni kwa hukumu na haki"

Atakuwa uthibiti katika nyakati zako

Hii inazungumzia Yahwe kusababisha watu wake kuwa imara kana kwamba alikuwa uthabiti mwenyewe. Msemo "nyakati zako" una maana ya maisha yao. "Atakufanya salama maisha yako yote"

wingi wa wokovu, hekima, na maarifa

Maneno ambayo hayapo yanaweza kuongezwa. Pia "wokovu" inaweza kuelezwa kwa kitenzi "okoa". "na atakupatia wingi wa wokovu, hekima, na maarifa" au "atakuokoa na kukupa wingi wa hekima na maarifa"

hofu ya Yahwe ni hazina yake

Hii inazungumzia kumhofu Yahwe kana kwamba ilikuwa hazina ambayo Yahwe hutoa kwa watu wake. "kumcha Yahwe itakuwa kama hazina yenye thamani ambayo atakupatia wewe" au "kumcha Yahwe itakuwa na thamani kwako kama hazina"

Isaiah 33:7

Tazama

Neno hilii lnatumika hapa kuvuta nadhari ya wtu kwa kile kinasemwa baadaye. Inatumika hapa pia kuweka alama kwa sehemu mpya katika kitabu. "Sikiliza"

wajumbe

"majumbe"

wanadiplomasia wenye matumaini ya amani hulia kwa uchungu

Hii na maana wanalia kwa sababu hawafanikiwi kutengeneza amani. "wanadiplomasia wanatumaini kwa ajili ya amani lakini hawafanikiwi na kwa hiyo wanalia kwa uchungu"

Barabara zimetelekezwa; hakuna wasafiri tena

Misemo hii miwili inasisitiza ya kwamba hakuna msafiri katika barabara. Hii inaweza kuunganshwa na kuandika katika hali ya kutenda. "Watu hawasafiri tena katika barabara".

Maagano yanavunjwa, mashahidi wanadharauliwa, na mwanadamu haheshimiwi

Mstari huu una maana ya hali za ujumla za uharibifu wa Israeli, au inaweza kumaanisha kutoweza kwa taifa kufanya makubaliano yanayoaminika ya amani na Ashuru. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Watu huvunja maagano ambayo wameyafanya, watu kutojali ushuhuda wa mashahidi, na watu kutojiheshimu wao kwa wao"

Isaiah 33:9

Nchi inaomboleza na kunyauka

Hii inazungumzia nchi kuwa kavu kana kwamba ilikuwa mtu anayeomboleza. "Nchi kuwa kavu na mimea yake kunyauka"

anaona aibu na ananyauka

Hii inazungumzia miti ya Lebanoni kunyauka na kuoza kana kwamba Lebanoni ilikuwa mtu ambaye ameaibika. "Miti ya Lebanoni hunyauka na kuoza"

Sharoni ... Bashani ... Karmeli

Miti mingi na maua iliwahi kuota katika maeneo haya.

Sharoni ni kama jangwa wazi

Hii inalinganisha jinsi Sharoni ilivyo kavu kwa jangwa wazi. "Sharoni ni kavu kama jangwa wazi"

Bashani na Karmeli hutikisa majani yao

"hakuna majani tena katika miti ya Bashani na Karmeli"

Isaiah 33:10

inuka

"simama". Hapa neno hili lina maana ya kuanza kufanya jambo. Katika hali hii Yahwe sasa anajinua mwenyewe.

sasa nitainuliwa; sasa nitapandishwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. Misemo hii miwili ina maana moja na inasisitiza Yahwe kuinuliwa. "sasa nitajiinua na kuonyesha ya kwamba ninastahili kwa ajili ya kila mtu kuniheshimu"

Unachukua mimba ya makapi, na unazaa mashina ya mabua

Hii inazungumzia Ashuru kufanya mipango kana kwamba walikuwa wakitunga mimba na kuzaa mipango yao kama mama anavyozaa mtoto. Hii inazungumzia mipango yao kutokuwa na thamani kwa kulinganisha na majani makavu. "Unafanya mipango ambayo haina thamani kama makapi na majani makavu"

mashina ya mabua

"majani makavu"

pumzi yako ni moto ambayo itakuangamiza

Hapa mipango ya Ashuru ina maana ya "pumzi" yao. Hii inazungumzia mipango yao kusababisha wao kufa kana kwamba mipango yao ingechoma miili yao kihalisia. "mipango yako itasababisha ufe"

Watu watachomwa mpaka kuwa chokaa, kama miiba ya vichaka inavyokatwa chini na kuchomwa

Hii inalinganisha jinsi maiti za watu itakavyochomwa kwa njia ambayo vichaka vya miiba inachomwa. Pia, hi inaweza kuandikwa katika hali ya kutenda. "Moto utachoma miili ya watu kuwa chokaa kwa nja moja ambayo mkulima hukata chini vichaka vya miiba na kuvichoma"

chokaa

mjivu kutoka kwa mifupa iliyoungua

Isaiah 33:13

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza

Wewe uliye mbali, sikiliza kile nilichofanya; na, wewe uliye karibu, kubali nguvu yangu

Yahwe anatumia maneno "mbali" na "karibu" kumaanisha watu wote. Neno "nguvu" linaweza kuelezwa kwa kivumishi "uwezo". "Watu wote kil sehemu watasikia kile nilichofanya na kukubali ya kwamba nina uwezo"

kutetemeka kumekamata wasio na Mungu

Hii inazungumzia watu wasio na Mungu kutetemeka kana kwamba kutetemeka kwao kulikuwa adui aliyewakamata. "wasio na Mungu wameingiwa kabisa na kutetemeka"

Nani kati yetu ... kuungua

Inadokvzwa ya kwamba mwenye dhambi wa Sayuni anauliza maswali haya. "Wanasema, 'Nani kati yetu ... kuungua"

Nani kati yetu anaweza kushindana na moto mkali? Nani kati yetu anaweza kushindana na kuungua kwa milele?

Maswali haya ya balagha yana maana moja na inasisitiza ya kwamba hakuna mtu anayeshi na moto. Hapa moto unwakilisha hukumu ya Yahwe. "Hakuna mtu anaweza kuishi kwa moto mkali! Hakuna mtu anaweza kuishi na moto wa milele!" au "Hakuna mtu anaweza kuishi kwa kubeba hukumu ya Yahwe, ni kama moto wa milele!"

kushindana

kuishi katiika eneo ambalo sio nyumba ya mtu

Isaiah 33:15

Yule anayetembea

Hapa kutembea ina maana ya kuishi. "Yule ambaye anaishi"

yule ambaye hudharau ongezeko la mali kwa dhuluma

Msemo wa nomino "ongezeko la mali kwa dhuluma" linaweza kuelezwa kama msemo wa kitenzi. "yule ambaye huchukia utajiri unaotokana na kudhuru watu wengine"

na haangalii uovu

"Kutazama" hapa ina maana ya kuidhinisha jambo. "na yule ambaye hakubaliani na kutenda uovu"

vilele

Hii ina maana ya kilima ch juu au upane wa mlima. "kilima cha juu" au "upande wa mlima"

ngome za miamba

Hii inazungumzia maeneo ya mawe ambayo ni rahisi kujilinda kana kwamba ilikuwa ngome kihalisia. "rundo kubwa la mawe"

itatolewa bila kikomo

"itakuwepo daima"

Isaiah 33:17

Macho yako yataona .. yatatazama

Hii ina maana ya watazamaji kwa "macho" yao. "Utaona ... utatazama"

mfalme katika uzuri wake

Majoho ya kifalme ya mfalme yanaelezwa kama "uzuri wake". "mfalme katika majoho yake mazuri"

Moyo wako utakumbuka hofu kuu

Hii ina maana ya watazamaji kwa "mioyo" yao. "Hofu kuu" ina maana ya vita yao na Ashuru. Hii inaweza kuandikwa wazi. "Utakumbuka hofu kuu ambayo Ashuru alisababisha kwako alipokushambulia"

yuko wapi mwandishi, yuko wapi yule ambaye alipima uzito wa fedha? Yuko wapo yule aliyehesabu minara?

Swali hili la balagha linaulizwa kusisitiza ya kwamba maafisa wa Ashuru wametoweka. Maswali haya yanweza kuandikwa kama kauli. "Maafisa wa Ashuru ambao walihesabu fedha za kodi ambayo ililazimishwa kulipwa kwao imepotea! Wanamume hao ambao walihesabu minara yetu wametoweka!"

alipima uzito wa fedha

Fedha ilikuwa chuma yenye thamani; uthamani wake ulithibitshwa kwa uzito wake.

watu wenye lugha ya ajabu

"watu ambao walizungumza lugha ya ajabu"

hamuwaelewi

"kuelewa"

Isaiah 33:20

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza na watu wa Yuda.

mji wa sikukuu zetu

Hii ina maana ya kwamba wana sikuku zao na sherehe katika mji. "mji ambapo tuna sikuku zetu" au "mji ambao tunasherehekea karamu zetu"

macho yako yataona

Watu wanajulikana kwa "macho" yao kusisitiza kile wanachoona. "utaona"

hema ambalo halitaondolewa

Hii inazungumzia Sayuni kuwa salama na kuimarishwa kana kwamba ilikuwa hema lililo salama. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda na kuandikwa kama sentensi mpya. "itakuwa salama, kama hema ambalo hakuna mtu atakayeliondoa kamwe"

ambalo viging vyake havitawah kuvutwa wala kamba zake kukatwa

Hii ni sehemu ya sitiari ambayo inalinganisha Sayuni kwa hema salama. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "ambalo vigingi hakuna mtu atawahi kuvivuta juu na ambalo kamba zake hakuna awezaye kuvikata"

Yahwe katika utukufu atakuwa pamoja nasi, katika sehemu ya mito mipana na vijito

Hapa "nasi" ina maana ya Isaya na inajumuisha watu wa Yuda. Hii inazungumzia usalama wa kuishi na Yahwe kana kwamba ilikuwa sehemu ambayo ina mito ikizunguka ili kwamba maadui wasiweze kuishambulia. "Yahwe ambaye ni mtukufu atakuwa pamoja nasi, na tutakuwa salama kana kwamba tupo katika sehemu inayozungukwa kwa mito mipana"

utausafiria

"utasafiri juu ya mto"

Isaiah 33:22

wetu ... atatuokoa

Hii ina maana ya Isaya na inajumlisha watu wa Yuda.

Isaiah 33:23

Kamba zako ni goigoi; haziwezi kushikilia mlingoti mkuu katika sehemu yake; hawawezi kulitandaza tanga

Maana zaweza kuwa 1) jeshi la Ashuru ni kama mtumbwi ambao hauwezi kusogea katikati ya maji: kamba ambazo hushikilia mlingoti mkuu na tanga zimekuwa legevu na hazishiki tena mlingoti mkuu, kwa hiyo tanga halina faida (33:1) au 2) watu wa Yuda hawapo vitani tena. "Umelegeza kamba ambazo zilishikilia nguzo zako za bender; bendera haipepei tena"

mlingoti mkuu

nguzo ndefu ambazo hushikilia tanga

tanga

kitambaa kikubwa ambacho hujazwa na upepo na kusogeza mtumbwi katikati ya maji

mali kubwa iliyoibiiwa itakapogawanywa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "watakapogawanya hazina"

vilema

Hii ina maana ya watu ambao hawawezi kutembea. "wale ambao ni vilema"

watu wanaoishi pale watasamehewa kwa udhalimu wao

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe atasamehe dhambi za watu wanaoishi pale"

Isaiah 34

Isaiah 34:1

Taarifa ya Jumla

Yahwe anazungumza katika shairi.

Dunia na kila kitu kinachoijaza wanapaswa kusikiliza, ulimwengu, na vitu vyote vitokanavyo nao

Hapa dunia inazungumziwa kama inahitajika kumsikiliza Yahwe kusisitiza ya kwamba ipo chini ya mamlaka ya Yahwe. Misemo hii miwili ya sambamba ni mifano ya maneno kwa ajili ya watu wote wanaoishi ulimwenguni. "Katika sehemu zote duniani, kila mtu anapaswa kusikiliz kile nachosema"

ulimwengu, na vitu vyote vitokanavyo nao

Hii ni misemo ya sambamba ya pili. Maneno ambayo hayapo yanaweza kuongezwa katika msemo huu. "ulimwengu, na vitu vyote viunavyotoka kutoka kwake vinapaswa kusikiliza"

ameyaangamiza kabisa, ameyakabidhi kwa ajili ya kuchinjwa

Mara kwa mara manabii huzungumzia vitu ambavyo vitatokea katika siku za usoni kana kwamba vimekwisha tokea. Hii inasisitiza tukio litatokea hakika. "atawaangamiza kabisa, atawakabidhi katika machinjo"

Isaiah 34:3

Miili ya wafu wao itatupwa nje

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Hakuna ambaye atazika wafu wao"

wafu wao

Hii ina maana ya watu waliokufa. "wale ambao wamekufa"

milima itafyonza damu yao

"milima itafunikwa katika damu yao"

mbingu itakunjwa kama hati ya kukunja

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. Hii inalinganisha kile ambacho Yahwe atafanya kwa mbingu kama mtu akikunja hati ya kukunja. "Yahwe atakunja hati ya kukunja kwa njia moja ambavyo mtu hukunja hati ya kukunja"

na nyota zao zote zitafifia, kama jani linavyofifia kutoka katika shina, na kama tini ilioiva kutoka kwenye mtini

Hii inasisitiza hata vitu katika mbingu ambavyo watu walidhani vingekuwa kule milele vitaanguka kwa urahisi kama jani. "na nyota zote zitaanguka kutoka mbinguni kama jani linavyoanguka kutoka katika shina au tini unavyoanguka kutoka katika mti"

Isaiah 34:5

pale upanga wangu utakapokuwa umekunywa ujazo wake mbinguni

Yahwe anajifafanua kama shujaa anayebeba upanga. Msemo "umekunywa ujazo wake" unazungumzia upanga wa Yahwe kana kwamba ulikuwa mtu ambaye amekula na kutosheka. Yahwe anatumia picha hii kusisitiza ya kwamba kutakuwa na uharibifu mwingi mbinguni na kutaja ukamilifu wake. "nitakapomaliiza kuangamiza vitu mbinguni"

tazama

Neno hili linatumika hapa kuwavuta wasikilizaji na kuwafanya wawaze mambo yanayosemwa. "sikiliza" au "na kisha"

sasa itashuka chini mpaka Edomu, juu ya watu naowaweka kando kwa ajili ya uharibifu

Neno "itashuka" ina maana ya upanga wa Yahwe. Hii inaendeleza sitiari kuhusu Yahwe kuangamiza vitu kwa upanga. "Nitakuja kuadhibu watu wa Edomu, watu ambao nimewaweka kando kwa ajili yangu kuangamiza"

juu ya Edomu

Edomu ina maana ya watu ambao wanaishi kule. "juu ya watu wa Edomu"

upanga wa Yahwe unadondoka kwa damu na kufunikwa na mafuta... wa kondoo dume

Hii inazungumzia Yahwe kuwaua watu kana kwamba alikuwa kuhani akitoa wanyama sadaka. Anafanya hivi kwa kufafanua upanga wa kuhani. "Yahwe anawatoa sadaka kama vile kuhani anavyotoa sadaka za wanyama, ambaye upanga wake unadondoka na damu na mafuta ya kondoo, mbuzi na kondoo dume"

Kwa maana Yahwe ana sadaka Bozra na machinjio makubwa katika nchi ya Edomu

Maneno "sadaka" na "machinjio" yanaweza kuelezwa hapa kama vitenzi. "

Bozra

Huu ni mji muhimu katika Edomu

Isaiah 34:7

Maksai pori watachinjwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Mimi, Yahwe nitachinja maksai pori"

Nchi yao italewa kwa damu

Hii inaelezea kiwango cha damu ambacho italowa katika ardhi kwa kulinganisha nchi na mtu mlevi. "Nchi yao italowa kwa damu"

vumbi lao lilifanya nono kwa unene

Hapa "vumbi" ina maana ya udongo juu ya ardhi. Hii inaelezea kiwango cha mafuta ambacho kitalowanisha katika udongo kwa kumlinganisha kwa mtu ambaye amenenepa kwa kula sana mafuta ya mnyama. "udongo utakuwa umejaa mafuta ya wanyama"

Isaiah 34:8

itakuwa siku ya kisasi kwa ajili ya Yahwe

Hapa "siku" ni lahaja kwa ajili ya kipindi katika wakati; sio "siku" halisi. "itakuwa wakati ambapo Yahwe atapata kisasi"

atawalipa kwa ajili ya Sayuni

Hii ina maana ya kwamba atachukua kisasi juu yao kwa jinsi walivyofanya vita kipindi cha nyuma dhidi ya watu wa Yerusalemu. "atawapa adhabu wanayostahili kwa kile walichofanya kwa watu wa Sayuni"

vijito vya Edomu vitageuzwa kuwa lami nyeusi ... kuwa lami inayowaka

Maji na nchi kutokuwa na thamani kwa ajili ya kunywa au kuotesha chakula kwa sababu imeungua na kufunikwa katika lami na salfa inazungumziwa kana kwamba vijito vyake na nchi itakuwa lami na salfa. "Vijito vya Edomu vitajaa lami na ardhi itafunikwa na salfa inayowaka na lami inayowaka"

vumbii lake ... nchi yake

"Vumbi la Edomu ... nchi ya Edomu"

lami

dutu nene, nyeusii ambayo inawaka kwa muda mrefu

itawaka usiku na mchana

Hii iina maana wakati wote. "Itawaka usiku wote na mchana" au "Itawaka kwa muendelezo, usiku wote na mchana wote"

kutoka kizazi mpaka kizazi

Msemo "kizazi mpaka kizazi" una maana ya vizazi vyote vya watu ambao wataishi katika siku za usoni.

Isaiah 34:11

wataishi kule

"wataishi katika nchi ya Edomu"

bundi

Bundi ni ndege pori wanaowinda usiku

kunguru

Huyu ni ndege mkubwa mweusi. Ni vigumu kutambua baadhi ya aina haswa za ndege zinazotajwa katika sehemu hii. Hata hivyo, wote walikuwa ndege ambao walipendelea kuishi katika maeneo ambayo hapakuwa na watu, kwa hiyo waliashiria sehemu zilizotelekezwa.

ndani mwake

"kule". Hii ina maana ya Edomu.

Naye atanyosha juu yake kamba ya kupimia ya uharibifu na timazi ya uvunjifu

Hii inamzungumzia Yahwe kana kwamba alikuwa mjenzi mwangalifu kama akisababisha uharibifu katika Edomu. "Yahwe atapima nchi kwa uangalifu; atapima kuamua wapi kusababisha uharibifu na uvunjifu"

kamba ya kupimia ... timazi

Hivi ni vifaa vya mjenzi.

Waadilifu wake ... wakuu wake

"Waadilifu wa Edomu ... wakuu wa Edomu"

wakuu wake wote hawatukuwa kitu

Hii inakuza kuhusu wakuu kupoteza nafasi yao ya ufalme kwa kusema watakuwa si kitu. "wakuu wake wote hawatatawala tena"

Isaiah 34:13

Miiba ... upupu ... mbaruti

Haya yote ni magugu yenye miiba. Miiba ya upupu ina sumu inayosababisha mwasho.

mbweha ... mbuni ... wanyama pori ... fisi ... Bundi ...

mbweha ... mbuni ... wanyama pori ... fisi ... Bundi

Wanyama wa usiku

Wanyama ambao wapo macho na wanashughulika usiku

mwewe

ndege ambao wanaua wanyama wadogo kwa ajili ya chakula

Isaiah 34:16

Tafuteni katika hati ya kukunja ya Yahwe

Msemo "hati ya kukunja ya Yahwe" ina maana ina ujumbe unaozungumzwa na Yahwe. "Soma kwa uangalifu kile kilichoandikwa katika hati hii ya kukunja ambayo ina ujumbe wa Yahwe"

hakuna moja kati hawa

"hakuna mmoja wa wanyama"

Hakuna mmoja wao atakosa mwenzi

Hii inaweza kuandikwa kama kauli chanya. "Kila mnyama atakuwa na mwenzi"

kwa maana kinywa chake kimeiamuru

Yahwe anatajwa kwa "kinywa" chake kusisitiza kile alichosema. "kwa maana Yahwe ameiamuru"

Amepiga kura kwa nafasi zao

Hii inazungumzia kuhusu Yahwe kuamua wapi kusababisha wanyama kuishi kana kwamba alipiga kura kihalisia kwa ajili ya sehemu zao. "Amekusudia wapi wataishi"

na mkono wake umepima kwa ajili yao kwa mkanda

Hii ina maana ya njia ambayo watu walipima viutu kipindi cha Biblia. "na amewapa wanyama sehemu zao"

kutoka kizazi mpaka kizazi wataishi

Msemo huu "kizazi mpaka kizazi" una maana ya vizazi vyote vya watu ambao wataishi katika siku za usoni. "milele wataishi" au "wataendelea siku zote"

Isaiah 35

Isaiah 35:1

Nyika na mahali penye ukiwa patafurahi; na jangwa litashangilia

Misemo hii miwili kimsingi iuna maana moja. Sehemu hizi inaelezwa kama kuwa na furaha, kama mtu anavyokuwa na furaha, kwa sababu zimepokea maji na zinachanua. "Itakuwa kama nyika na mahali penye ukiwa pana furaha na jangwa litashangilia"

na kuchanua

Hii inazungumzia mimea katika jangwa kuchanua kana kwamba jangwa lenyewe lilikuwa likichanua. "na mimea yake itachanua"

Kama waridi, litachanua kwa wingi

Hii inalinganisha namna ya mimea ya jangwa huchanua kwa namna ambavyo waridi unavyochanua kwa wingi. "Jangwa litaota mimea na miti mipya mingi"

na kushangilia kwa furaha na kuimba

Hii inazungumzia jangwa kana kwamba ilikuwa na furaha na kuimba kama mtu. "itakuwa kana kwamba kila kitu kinashangilia na kuimba!"

utukufu wa Lebanoni utapewa kwake

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. Hii inazungumzia Yahwe kulifanya jangwa kuonekana na utukufu kama wa Lebanoni kana kwamba alikuwa akilipa jangwa utukufu wa Lebanoni. "Yahwe ataupatia Lebanoniu utukufu wake" au "Yahwe ataufanya uwe mzuri kama Lebanoni"

uzuri wa Karmeli na Sharoni

Maneno ambayo hayapo yanaweza kuongezwa. Pia, hii inamzungumzia Yahwe kulifanya jangwa kuonekana zuri kama Karmeli na Sharoni kana kwamba alikuwa akilipa jangwa uzuri wake. "uzuri wa Karmeli na Sharoni utapewa kwake" au "Yahwe ataufanya uwe mzuri kama Karmeli na Sharoni"

utukufu wa Yahwe, uzuri wa Mungu wetu

Misemo hii miwili kimsingi ina maana moja na inasisitiza kutokea kwa Yahwe.

Isaiah 35:3

Taarifa ya Jumla

Isaya anazungumza na watu wa Yuda.

Imarisha mikono iliyolegea, na nyosha magoti yanayotetemeka

Maneno "mikono iliyolegea" na "magotiu yanayotetemeka" yanawakilisha mtu ambaye ana hofu. "Imarisha wale ambao mikono yao ni dhaifu na ambao magoti yao hutetemeka kwa hofu"

wale wenye moyo wa uoga

Hapa watu wanamaanishwa kwa mioyo yao, ambayo inasisitiza hisia zao za ndani. "kwa wale ambao wana hofu"

Tazama

Hii ni lahaja. Neno hili linatumika hapa kuwavuta wasikilizaji kwa kile kinachosemwa baadaye. "Sikilizeni"

Mungu wako atakuja na kisasi, kwa fidia ya Mungu

Hii inaweza kusemwa kwa neno lingine ili kwamba nomino dhahania "kisasi" na "fidia" inaelezwa kama kitenzi "adhibu". Maneno haya "kisasi" na "fidia" yana maana moja na yanasisitiza ya kwamba Mungu atawaadhibu maadui wa Yuda. "Mungu wako ataadhibu adui zako kwa kile walichokifanya"

Isaiah 35:5

Taarifa ya Jumla

Mistari hii inaanza maelezo ya utukufu ujao wa watu wa Mungu.

macho ya vipofu yataona

"Vipofu" ina maana ya watu ambao ni vipofu. Wanamaanishwa kwa "macho" yao kusisitiza uponyaji wao. "watu vipofu wataona"

masikio ya viziwi yatasikia

"Viziwi" ina maana wa watu ambao hawawezi kusikia. Wanamaanishwa kwa "masikio" yao kusisitiuza uponyaji wao. "watu viziwi watasikia"

mtu kilema ataruka kama mbawala

Hii ina maana mtu ambaye hawezi kutembea ataweza kuruka. Uwezo wake kuruka inakuzwa kwa kusema ya kwamba anaweza kuruka kama mbawala. "mtu kilema ataruka juu"

ulimi usiozungumza utaimba

Hii ina maana ya watu ambao hawawezi kuongea. Wanamaanishwa kwa "ndimi" zao kusisitiza uponyaji wao. "bubu wataimba"

vijito katika nyika

Maneno ambayo hayapo yanaweza kuongezwa. "vijito vitatiririka katika nyika"

mchanga unaochoma utakuwa dimbwi

Hii ina maana ya kwamba dimbwi la maji litajitokeza katika mchanga wa moto. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "Dimbwi litajitokeza katika mchanga unaochoma"

ardhi yenye kiu

Hapa ardhi kavu inaelezwa kama kuwa na kiu. "ardhi iliyokauka"

ardhi yenye kiu kuwa chemchemi za maji

Hii ina maana ya kwamba chemchemi itajitokeza katika ardhi ngumu. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "chemchemi za maji zitatokea katika ardhi yenye kiu"

mbweha

mbwa mwitu

mafunjo na matete

Hii ni mimea ambayo huota katika maeneo yaliyoloana.

Isaiah 35:8

Taarifa ya Jumla

Mistari hii naendeleza ufafanuzi wa utukufu ujao wa watu wa Mungu.

Barabara itakuwa pale inayoitwa Njia Takatifu

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Barabara itakuwa pale ambayo iatkuwa na jina Njia Takatifu"

barabara

Mtoto mdogo atawatunza na kuwaongoza katika sehemu nzuri kunywa maji na kula nyasi.

wachafu

Hii ina maana ya watu wasio safi. Mtu ambaye Mungu humchukulia kutokubalika kiroho au najisi anazungumziwa kana kwamba mtu alikuwa mchafu kimwili. "Wale ambao na wachafu" au "Watu ambao hawakubaliki kwa Mungu"

yule atembeaye ndani yake

Hii ni lahaja. Hapa "kutembea" ina maana ya "kuishi". Hii ina maana ya mtu ambaye anaishi maisha matakatifu. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "yule ambaye anaishi katika njia ya utakatifu" au "yule ambaye huishi maisha ya utakatifu"

hawatapatikana pale

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "hakuna mtu atakayewakuta kule"

waliokombolewa

Hii ina maana ya watu ambao Mungu amewakomboa. "wale ambao wamekombolewa" au "wale ambao Mungu kawakomboa"

Isaiah 35:10

Waliofidiwa wa Yahwe

"kufidia" ina maana ya "kukoa". Hii ina maana ya watu ambao Yahwe kawakomboa. "Wale ambao Yahwe amewaokoa"

furaha ya milele itakuwa juu ya vichwa vyao

Hii inatumia kichwa cha mtu kumaanisha mtu kwa ujumla. "watakuwa na furaha ya milele"

furaha na shangwe ... huzuni na tanafusi

Maneno "furaha" na "shangwe" kimsingi ina maana moja, kama vile "huzuni" na "kutanafusi". Kwa pamoja yanasisitiza mkazo wa hisia hizi.

furaha na shangwe itawapita wao

Hii inazungumzia watu kushindwa kabisa na furaha na shangwe kwa kuzipatia hisia hizi sifa za kibinadamu ya kuweza kumpita mtu kwa lazima. "watashindwa kabisa kwa shangwe na furaha"

huzuni na tanafusi itatoroka

Hii inazungumzia juu ya watu kutokuwa na huzuni na kutanafusi kwa kuzipa hisia hizi uwezo wa kibinadamu wa kukimbia. "hawatakuwa na huzuni na kutanafusi"

Isaiah 36

Isaiah 36:1

mwaka wa kumi na nne

"mwaka wa 14"

Mfalme Hezekia

Hezekia alikuwa mfalme wa Yuda

Senakeribu

Hili ni jina la mfalme wa Ashuru.

Senakeribu ... alishambulia miji yote iliyoimarishwa

Jeshi la Senakeribu lilivamia miji. "Senekeribu na jeshi lake ... walivamia miji yote iliyoimarishwa"

kamanda mkuu

Baadhi ya tafsiri za Biblia zinatafsiri kuwa hii ni ""Rabshake". Hili ni neno la Ashuru kwa yule mwenye nafasi ya juu kabisa ya viongozi wa kijeshi Ashuru.

Lakishi

Huu ni mji kusini magharibi mwa Yerusalemu.

mfereji wa dimbwi la juu katika barabara ya kuelekea shamba la dobi

"ambapo maji huingia katika dimbwi la juu"

Hilkia ... Eliakimu

Haya ni majina ya wanamume.

Shebna

Hili ni jina la msimaizi wa kasri ya mfalme Yerusalemu

Asafu ... Yoa

Haya ni majina ya wanamume.

Isaiah 36:4

akasema kwao

"akasema kwa Eliakimu, Shebna, na Yoa"

Chanzo cha matumaini yenu ni nini?

Mfalme wa Ashuru anatumia swali hili kutoa changamoto kwa Hezekia na kusema ya kwamba hana chanzo kizuri cha imani. Swali hili linaweza kuandikwa kama kauli. "Hauna chanzo cha kutegemea cha imani yako"

kuna ushauri na nguvu kwa ajili ya vita

"una ushauri na nguvu ya kwenda vitani". Msemo "nguvu kwa ajili ya vita" ina maana ya kuwa na jeshi kubwa la kutosha na la nguvu ya kutosha yenye silaha. "una ushauri wa kijeshi wa kutosha, wanamume wenye nguvu, na silaha za kwenda vitani"

Basi sasa ni nani mnayemwamini? Ni nani kawapa ujasiri kuasi shidi yangu?

Mfalme wa Ashuru anatumia maswali kumdhihaki Hezekia kwa kuamini ya kuwa ana nguvu ya kuasi. Swali hili linaweza kuandikwa kama kauli. "Haijalishi unamwamini nani, hautakuwa na ujasiri wa kuasi dhidi yangu".

Isaiah 36:6

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza ujumbe wa mfalme wa Ashuru kwa Hezekia. Kamanda mkuu anazungumza ujumbe kwa wanamume wa Hezekia.

Tazama

Senakeribu anatumia lahaja kumvuta Hezekia kwa kile anachotaka kusema hivi punde.

unamtegemea Misri

Hapa "Misri" ina maana ya jeshi la Misri. "kuamini katika jesgi la Misri"

hilo tete lililochanikachanika ambalo unatumia kama gongo la kutembelea, lakini kama mtu akaliegemea, litaganda mkononi mwake na kuuchuma

Hii inazungumzia Misri, haswa jeshi lake na Farao wake, kana kwamba lilikuwa tete lililochanikachanika kusisitiza ya kwamba kuwategemea hakuwezi kuwasaidia lakini kutawadhuru tu. "hiyo ni kama kutembea kwa tete lililochanikachanika kwa ajili ya gongo. Kama mtu ataliegemea, litanga'ang'ani kwenye mkono wake na kuuchoma"

tete lililochanikachanika

tete ni shina refu la mmea kama nyasi ndefu. Kama limechanikachanika au kuharibika haliwezi kubeba uzito wowote.

gongo la kutembelea

Hiki ni kijiti ambacho mtu anaweza kutumia kama mhimili anapotembea, kimetengenezwa kwa mti wa aina yoyote ambao hukutwa njiani.

je! yeye siye yule ambaye sehemu zake za juu na madhabahu zimeondolewa na Hezekia ... Yerusalemu"?

Mfalme wa Ashuru anatumia swali hili kudhihaki watu na kuonyesha ya kwamba Yahwe alikuwa amekasirika juu ya Hezekia alichofanya na asingewalinda. Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "yeye ndiye ambaye sehemu zake za juu na madhabahu yameondolewa na Hezekia ... Yerusalemu" au "yeye ndiye ambaye sehemu zake za juu na madhabahu ... Yerusalemu".

akamwambia Yuda na Yerusalemu, "Unatakiwa kuabudu mbele ya dhabahu hili katika Yerusalemu"?

Hii inaweza kuandikwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Yuda" na "Yerusalemu" ina maana ya watu ambao wanaishi humo. "amewaambia watu wa Yuda na Yerusalemu ya kwamba wanapaswa kuabudu katika dhabahu hili tu Yerusalemu"

Isaiah 36:8

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza ujumbe wa mfalme wa Ashuru kwa Hezekia kwa kuzungumnza ujumbe kwa wanamume wa Hezekia.

farasi elfu mbili

"farasi 2,000"

kama unaweza kupata wafunza farasi kwa ajili yao

Kamanda mkuu anaendelea kumdhihaki Hezekia na jeshi lake kwa kudokeza ya kwamba hakuwa na wanajeshi wengi.

Isaiah 36:9

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza ujumbe wa mfalme wa Ashuru kwa Hezekia kwa kuzungumnza ujumbe kwa wanamume wa Hezekia.

Unawezaje kumpinga hata nahodha mmoja ... watumishi?

Kamanda mkuu anaendelea kumdhihaki Hezekia na jeshi lake. Anaposema "unawezaje" kumaanisha Hezekia, kihalisia anamaanisha jeshi la Hezekia. Swali hili linaweza kuandikwa kama kauli. "Jeshi lako hata haliwezi kushinda nahodha mmoja ...watumishi".

Basi sasa, sijasafiri hapa bila Yahwe kupigana dhidi ya nchi hii na kuiangamiza?

Kamanda mkuu anatumia swali lingine kumdhihaki Hezekia na watu wa Yuda. swali hili linaweza kuandikwa kama kauli. "Nilikuja hapa pamoja na amri ya Yahwe kuangamiza Yerusalemu"

bila Yahwe

Hapa "Yahwe" ina maana ya amri za Yahwe. "bila amri ya Yahwe"

dhidi ya nchi hii na kuiangamiza ... Shambulia nchi hii na uiangamize

Hii ina maana kupigana dhidi ya watu na kusababisha uharibifu katika eneo ambalo wanaishi. Nchi inamaanishwa hapa ni Yerusalemu. "dhidi ya watu hawa na kuangamiza nchi yao ... Shambulia watu hawa na angamiza nchi yao"

Isaiah 36:11

Eliakimu ... Hilkia ... Shebna

Haya ni majina ya wanamume.

Shebna

Hili ni jina la msimaizi wa kasri ya mfalme Yerusalemu

Yoa ...kamanda mkuu

Yoa ni jina la mwanamume. Kama mkuu ni mwenye nafasi ya juu kabisa ya viongozi wa kijeshi Ashuru.

Tafadhali zungumza kwa mtumishi wako

Eliakimu, Shebna, na Yoa wanajitambulisha kama watumishi wa makamanda wakuu. Hii njia ya upole ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka ya makubwa.

lugha ya Kiashuri, Kiyahudi

"Ashuru" ni jina la kundi la watu. "Kiashuri" ni jina la lugha yao

masikioni mwa watu ambao wapo katika ukuta

Lahaja "kuzungumza katika masikio ya mtu" ina maana ya kuzungumza pale ambapo watasikia. "ambapo watu walio juu ya ukuta waweze kutusikia"

ambao wapo katika ukuta

Hii ina maana wanasimama katika ukuta. Juu ya ukuta palikuwa papana na sehemu ambayo watu wanaweza kukaa au kusimama. Maana kamili inaweza kuwekwa wazi. "ambao wanasimama juu ya ukuta"

Je! bwana wangu amenituma kwa bwana wako na kwako kuzungumza maneno haya?

Kamanda mkuu anatumia swali hili kusisitiza ya kuwa ujumbe huu ni kwa ajili ya watu wote wa Yuda. Swali hili linaweza kuandikwa kama kauli. "Hakika, bwana wangu amenituma kuzungumza ujumbe huu kwako na wote wanaoweza kuusikia".

Je! hajanituma kwa wanamume ambao wanakaa juu ya ukuta, ambao ... wewe?

Kamanda mkuu anatumia swali hili kusisitiza tusi lake. "Bwana wangu amenituma kwa kila mmoja anayesikia hili, ambaye atapaswa ... wewe".

watapaswa kula kinyesi chao wenyewe na kunywa mkojo wao wenyewe pamoja na wewe

Hii ni kauli ya kuchukiza sana. Anadokeza ya kwamba watahitaji kula vitu hivi kwa sababu hawatakuwa na kitu kingine kula kwa sababu mji wao utashambuliwa. "hivi punde watahitaji kula kinyesi chao wenyewe na kunywa mkojo wao wenyewe, kama utakavyofanya, kwa sababu hautakuwa na kitu chochote cha kula"

Isaiah 36:13

kamanda mkuu

Baadhi ya tafsiri za Biblia zinatafsiri kuwa hii ni "Rabshake". Hili ni neno la Ashuru kwa yule mwenye nafasi ya juu kabisa ya viongozi wa kijeshi Ashuru.

mji huu hautakabidhiwa mikononi mwa mfalme wa Ashuru

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe hatawapatia Yerusalemu katika mkono wa mfalme wa Ashuru"

mkono wa mfalme

"mkono" wa mfalme una maana ya "utawala" wake. "utawala wa mfalme"

Isaiah 36:16

Maelezo ya Jumla

Kamanda mkuu anaendelea kuzungumza na watu wa Yuda.

Fanya amani na mimi

Lahaja hii ina maana ya kukubali rasmi kutenda kwa amani kwa mtu mwingine. "Tukubaliane kuwa na amani"

jitokeze uje kwangu

Lahaja hii ina maana ya kujisalimisha. "jisalimishe kwangu"

hadi ntakapokuja na kuchukua

Hapa mfalme wa Ashuru anamaanihsa kwa jeshi lake kama yeye mwenyewe. "hadi jeshi langu litakapokuja na kuchukua"

nchi ya nafaka na divai mpya, nchi ya mkate na mashamba ya mizabibu

Misemo hii miwili ina maana moja na inatumika pamoja kwa ajili ya msisitizo jinsi nchi itakavyokuwa na mafanikio.

nchi ya nafaka ... nchi ya mkate

Hii ina maana ya kwamba nchi imejaa rasilimali, kama vile nafaka. "nchi ambapo kuna nafaka nyingi ... nchi ambapo kuna mkate mwingi"

Isaiah 36:18

Taarifa ya Jumla

Kamanda mkuu anaendelea kuzungumza ujumbe wa mfalme wa Ashuru kwa watu wa Yuda.

Je! kuna miungu yoyote ya watu iliyowaokoa kutoka .... Ashuru?

Kamanda mkuu anatumia swali hili kudhihaki watu wa Yuda. Swali hili linaweza kuandikwa kama kauli. "hakuna kati ya miungu ya watu iliyowaokoa wao kutoka .... Ashuru"

mkono wa mfalme

Utawala wa mfalme una maana ya "mkono" wake. "utawala wa mfalme"

Wako wapi miungu wa Hamathi na Arpadi? Wako wapi miungu wa Sefarvaimu? Je! wameokoa Samaria kutoka katika nguvu yangu?

Kamanda mkuu anatumia maswali haya kudhihaki watu wa Yuda. Maswali haya yanaweza kuunganishwa na kuandikwa kama kauli. "Miungu ya hamathi, Arpadi, Sefravaimu, na Samaria haikuokoa watu wao kutoka katika nguvu yangu"

Hamathi ... Arpadi

Haya ni majina ya miji.

Sefarvaimu

Hili ni jina la mji.

Je! kuna mungu yeyote ambaye amekuokoa ... kana kwamba Yahwe anaweza kuokoa Yerusalemu kutoka katika nguvu yangu?

Kamanda mkuu anatumia swali hili kudhihaki watu wa Yuda. Swali hili linaweza kuandikwa kama kauli. "Hakuna mungu ambaye amekuokoa ... na Yahwe hatakuokoa Yerusalemu kutoka katika nguvu yangu"

nchi yake

Hii ina maana ya watu ambao wanaishi katika nchi. "watu wake"

Isaiah 36:21

Eliakimu ... Hilkia ... Sheban ... Yoa ... Asafu

Haya ni majina ya wanamume.

juu ya nyumba

Lahaja hii ina maana ya kwamba alikuwa msimamizi wa masuala ya kasri. "msimamizi wa kasri"

kwa nguo zao zilizochanika

maafisa wa Hezekia walichana nguo zao kama ishara ya kuomboleza na mateso. Maana ya hii inaweza kuwekwa wazi. "huku nguo zao zikiwa zimechanika kwa sababu walikuwa na wameteseka sana"

Isaiah 37

Isaiah 37:1

Ikaja kuwa kwamba

Msemo huu unatiwa hapa kuweka alama kwa tukio muhimu katika simulizi.

alichana nguo zake, akajifunika kwa nguo ya gunia

Hii ni ishara ya kuomboleza na dhiki. "alichana nguo zake na kujifunika kwa nguo ya gunia kwa sababu alikuwa na dhiki sana"

Eliakimu ... Shebna

Haya ni majina ya wanamume.

juu ya nyumba

Hii ni lahaja ambayo ina maana ya kwamba alikuwa akisimamia masuala ya kasri ya nyumba. "aliyesimamia kasri"

wote wakajifunika na nguo ya gunia

Hii ni ishara ya kuomboleza na kuhuzunika.

Isaiah 37:3

Walisema kwake

"Wanamume waliotumwa na Hezekia walisema kwa Isaya"

kama pale ambapo mtoto yupo tayari kuzaliwa, lakini mama hana nguvu ya kuzaa mtoto wake

Kulinganisha huku kunafanywa kusisitiza ya kwmba wapo katika kipindi kigumu sana. "Ni mateso kama siku ambapo mtoto yupo tayari kuzaliwa, lakini mama hana nguvu ya kuzaa mtoto wake"

Inaweza kuwa pale ambapo Yahwe Mungu wako atasikia maneno

Hezekia anadokeza sio moja kwa moja ya kwamba kama watu wataomba Yahwe anaweza kusikiliza na kutenda juu ya kile kamanda mkuu alichosema. Maana kamili ya kauli hii inaweza kufanywa wazi. "Huenda kama ukiomba kwa Yahwe Mungu wako atasikia ujumbe"

kamanda mku

Baadhi ya tafsiri za Biblia zinatafsiri kuwa hii ni ""Rabshake". Hili ni neno la Ashuru kwa yule mwenye nafasi ya juu kabisa ya viongozi wa kijeshi Ashuru.

bwana wake

Msemo huu una maana ya kwamba mfalme ni bwana wa kamanda mkuu.

na atakemea maneno ambayo Yahwe Mungu wako ameyasikia

Hapa msemo "maneno ambayo Yahwe Mungu wako amesikia" ina maana ya kile mfalme wa Ashuru amesema. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "na Yahwe Mungu wako atakemea mfalme wa Ashuru kwa kile alichosema"

inua maombi yako

Kuomba kwa Yahwe inaelezwa kwa njia hii kusisitiza ya kwamba Yahwe yupo mbinguni. Maombi yanazungumziwa kana kwamba yalikuwa vitu ambavyo vinaweza kuinuliwa juu angani. "omba"

kwa aliyesalia ambaye bado yupo pale

Hii ina maana ya watu ambao wamebaki Yerusalemu. "kwa wachache wetu ambao bado tupo hapa"

Isaiah 37:5

Nitaweka roho ndani yake, naye atasikia taarifa fulani na kurudi katika nchi yake

Msemo huu "kuweka roho ndani yake" ina maana ya kwamba Mungu atamshawishi kufanya maamuzi bayana. Neno "roho" hapa lina maana ya mtazamo wa nguvu au hisia. "Nitamshawishi ili kwamba atakaposikia taarifa fulani, atarudi katika nchi yake mwenyewe"

Tazama

Neno hili ni lahaja na linatumika hapa kuvuta nadhari ya watu kwa kile kinachosemwa baadaye. "Sikiliza"

Nitamsababisha aanguke kwa upanga katika nchi yake mwenyewe

Msemo "kuanguka kwa upanga" ni lahaja ambayo ina maana ya kwamba adui yake atamuua kwa upanga. "Na pale katika nchi yake mwenyewe, nitasababisha adui zake kumuua kwa panga zao"

Isaiah 37:8

Lakishi

Huu ni mji kusini magharibi mwa Yerusalemu.

Senakeribu

Hili ni jina la mfalme wa Ashuru.

Libna

Huu ni mji kusini mwa Yuda.

Tirhaka mfalme wa Ethiopia na Misri wamehasamisha kupigana dhidi yao

"Tirhaka" ni jina la mwanamume. Aliwahamasisha jeshi lake ili wawe tayari kupigana. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "Tirhaka mfalme wa Ethiopia na Misri alihamasisha jeshi lake"

kupigana dhidi yake

Neno "yake" inawakilisha Senakeribu. Msemo huu una maana ya kupigana dhidi ya jeshi la Senakeribu"

Yerusalemu haitatolewa katika mkono wa mfalme wa Ashuru

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. Neno "mkono" lina maana ya nguvu ya kijeshi ya mfalme. "Mfalme wa Ashuru na jeshi lake halitakushinda katika Yerusalemu"

Isaiah 37:11

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza ujumbe wa mfalme wa Ashuru kwa Hezekia.

Tazama, umesikia

Hii ni lahaja. Neno "tazama" hapa linatumika kuongeza msisitizo kwa kile kinachosemwa baadaye. "Hakika umesikia"

Kwa hiyo utakombolewa?

Mfalme wa Ashuru anatumia swali hili kumdhihaki Hezekia na jeshi lake. Hii inaweza kuandikwa kama kauli. "Kwa hiyo na wewe hautaokolewa" au "Kwa hiyo hakuna mtu atakayekuokoa pia!"

Je! miungu wa mataifa wamewaokoa ... Telasari?

Mfalme wa Ashuru anatumia swali hili kumdhihaki Hezekia na jeshi lake. Hii inaweza kuandikwa kama kauli. "Miungu ya mataifa hawakukomboa mataifa ambayo baba zangu waliangamiza ... Telasari!"

ambayo baba zangu waliangamiza

Wanamume hawa waliangamiza miji iliyoorodheshwa kwa kuishinda kwa majeshi yao. Hapa neno "baba" ina maana ya baba yake na babu zake wengine ambao walikuwa wafalme. "ambao baba zangu waliangamiza kwa majeshi yao"

Gozani ... Harani .... Resefu ... Adini ... Telasari ... Hena ... Iva

Hizi ni sehemu ambazo Ashuru alizishinda.

Yuko wapi mfalme ... Iva?

Mfalme wa Ashuru hutumia swali hili kumkejeli Hezekia na jeshi lake. Hii inaweza kuandikwa kama kauli. "Pia tulimshinda mfalme ... Iva!"

Hamathi ... Arpadi ... Sefarvaimu

Haya ni majina ya miji.

Isaiah 37:14

katika mkono wa wajumbe

Hapa wajumbe wanamaanishwa kwa "mkono" wao kusisitiza ya kwamba walimpatia mfalme wao binafsi. "ambayo wajumbe walimpatia"

akaelekea juu katika nyumba ya Yahwe

Nyumba ya Yahwe ilikuwa katika sehemu ya juu Yerusalemu, kwa hiyo inazungumziwa kama "juu".

kuikunjua mbele yake

"kuikunjua barua mbele ya Yahwe". Kuwa katika nyumba ya Yahwe inachukuliwa sawa na kuwa katika uwepo wa Yahwe. Barua ilikuwa hati ya kukunja ambayo inaweza kufunulia na kutandikwa.

wewe unayekaa juu ya makerubi

Hapa Hezekiia anazungumza kuhusu Yhwe kuwepo ndani ya hekalu. Maana ya hii inaweza kuwekwa wazi. "wewe ambaye upo hapa pamoja na makerubi"

wewe ni Mungu pekee

"wewe tu ni Mungu"

juu ya falme zote

Lahaja hii ina maana ya kuwa na mamlaka na kutawala juu ya falme zote. "kuwa na mamlaka juu ya falme zote"

Ulitengeneza mbingu na dunia

Hii ina maana ya kwamba aliumba kila kitu. "Uliumba kila kitu"

Isaiah 37:17

Taarifa ya Jumla

Hezekia anaendelea kuomba kwa Yahwe.

ambaye alimtuma

Hezekia anamaanisha barua kutoka kwa Senakeribu. Maana ya hii inaweza kuwekwa wazi. "katika ujumbe aliotuma"

Geuza sikio lako

"Tega sikio lako" au "Geuza kichwa chako". Hii ina maana kugeuza kichwa chako ili kwamba uweze kusikia jambo vizuri.

Senakeribu

Hili ni jina la mfalme wa Ashuru.

mataifa yote na nchi zao

Huku ni kukuza. Wafalme walikuwa wameangamiza nchi nyingi za karibu, lakini sio nchi zote. "mataifa mengi na nchi zao"

Isaiah 37:19

Taarifa ya Jumla

Hezekia anaendelea kuomba kwa Yahwe.

kwa maana hawakuwa miungu lakini kazi ya mikono ya watu, mabao na mawe tu

Hii inasisitiza ya kwamba wanadamu walifanya sanamu hizi kwa mikono yao wenyewe na kwa hiyo hazina thamani. "kwa sababu ilikuwa miungu ya uongo ambayo watu walitengeneza kwa mbao na mawe"

kutoka katika nguvu yake

"kutoka kwa mfalme wa nguvu ya Ashuru"

falme zote

Hii ina maana ya watu katika falme. "watu wote katka falme"

wewe ni Yahwe pekee

"wewe tu, Yahwe, ni Mungu"

Isaiah 37:21

akatuma ujumbe

Hii ina maana ya kwamba alituma mjumbe kutoa ujumbe kwa mfalme. "alimtuma mtu kutoa ujumbe"

ni neno ambalo Yahwe amenena

"ni kile Yahwe ambacho alisema"

anakucheka kwa kubeza

"anakucheka" au "kukudhihaki"

anatikisa kichwa chake

Hii ni ishara ya dharau.

Binti bikira wa Sayuni ... binti wa Yerusalemu

Hizi ni lahaja. Misemo hii miwili ina maana moja. "binti" wa mji ina maana watu ambao wanaishi katika mji huo. "Watu wa Sayuni ... watu wa Yerusalemu"

Ni nani umemkataa na kumtukana? ... Dhidi ya Mtakatifu wa Israeli

Yahwe anatumia maswali haya ya balagha kumkejeli mfalme wa Ashuru. Hii inaweza kuandikwa kama kauli. "Umemkataa na kumtukana Yahwe, umepiga kelele na kutenda kwa kiburi dhidi ya Mtakatifu wa Israeli!"

umeinua sauti yako

Hii ina maana ya kuongea kwa sautii kana kwamba sauti ya mtu ilikuwa kitu ambacho walikiinua juu. "je! umepiga kelele"

kuinua macho yako kwa kiburi

Hii ni lahaja ambayo ina maana ya kutazama kitu kwa kiburi, kujichukulia muhimu zaidi kuliko unavyotakiwa. "kutazama kwa kiburi" au "alitenda kwa kiburi"

Isaiah 37:24

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza ujumbe wa Yahwe kwa mfalme wa Ashuru

Kwa watumishi wako

Hii ina maana ya watumishi ambao aliwatuma kwa Hezekia na ujumbe. Hii inaweza kuwekwa wazi. "Katika ujumbe uliotuma na watumishi wako"

Nimekwenda ... Nitakata... Nitaingia ... Nmechimba ... Nilikausha ... miguu yangu

Hapa Senakeribu anajizungumzia kushinda vitu vingi. Kiuhalisia anawashinda kwa majeshi yake na vibandawazi. "Tumekwenda ... Tutakata ... Tutaingia ... Tumechimba ... Tulikausha ... miguu yetu"

mierezi yake mirefu

"mierezi mirefu ya Lebanoni"

misitu yake inayozaa zaidi

Hapa neno "inayozaa" ina maana ya msitu kuwa mzito na kujaa miti yenye afya. Maneno ambayo hayapo yanaweza kuongezwa kufanya maana kuwa wazi. "na katika msitu wake unaozaa zaidi"

Nilikausha mito yote ya Misri chini ya nyayo za miguu yangu

Hapa Senakeribu anakuza ushindi wake na kusafiri kupitia mito ya Misri kwa kudai kukausha mito alipotembeza jeshi lake mtoni. "Nimetembeza katikati ya mito yote ya Misri kana kwamba ilikuwa nchi kavu chini ya miguu yangu"

Isaiah 37:26

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza ujumbe wa Yahwe kw mfalme wa Ashuru.

Je! haujasikia jinsi ... nyakati?

Yahwe anatumia swali hili la balagha kumkumbusha Senakeribu kuhusu taarifa ambayo alipaswa kuwa anaifahamu. Hii inaweza kuandikwa kama kauli. "Hakika mmesikia jinsi ... nyakati".

Upo hapa kupunguza miji isioingilika katika marundo ya uharibifu

Yahwe alikuwa amepanga kwa jeshi la Senakeribu kuangamiza miji ambayo walikuwa wameangamiza. Hii inaweza kuwekwa wazi zaidi. "Nilipanga ya kwamba jeshi lako lingeangamiza miji na kuisababisha kuwa rundo la kifusi"

isioingilika

imara na yenye ulinzi mkali

wenye nguvu ndogo

"ambao ni dhaifu"

wamepondwapondwa

"kuvunjwa moyo"

Ninaifanya itimie

Lahaja "kufanya kitu kutimia" ina maana ya kusababisha kitu dhahiri kutokea. "Ninasababisha itokee" au "Ninasababisha vitu hivi kutendeka"

Wao ni mimea katika shamba, nyasi za kijani, nyasi juu ya paa au katika shamba, mbele ya upepo wa mashariki

Hii inazungumzia jinsi miji ilivyo dhaifu na kutoweza kujilinda mbele ya jeshi la Ashuru kwa kulinganisha miji na nyasi. "Miji ni dhaifu kama nyasi katika mashamba mbele ya majeshi yako. Wao ni dhaifu kama nyasi ambayo huota juu ya paa za nyumba na kuchomwa na upepo mkali wa mashariki"

upepo wa mashariki

Upepo wa mashariki ni wa moto na mkavu kutoka katika jangwa na mimea hufa unapovuma.

Isaiah 37:28

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza ujumbe wa Yahwe kwa mfalme wa Ashuru.

Lakini ninajua kukaa kwako chini, kutoka kwako, kuingia kwako

Hii ina maana ya vitendo vyote vya maisha. "Ninajua kila kitu unachofanya"

na hasira yako dhidi yangu

Neno "hasira" linaweza kuelezwa kama kitenzi. "jinsi unavyokasirika dhidi yangu"

kiburi chako

Hapa "kiburi" cha mfalme kina maana ya maneno yake ya kiburi. "maneno yako ya kiburi"

kiburi chako kimeyafikia masikio yangu

Hii inazungumzia yahwe kusikia maneno ya mfalme kana kwamba maneno ya mfalme yalikuwa kitu ambacho kilisafiri mpaka katika sikio lake. "Nimesikia ukizungumza kwa kiburi"

nitaweka ndoano yangu katika pua yako, na lijamu katika mdomo wako

Mtu hutumia ndoano na lijamu kuongoza mnyama. Hii inazungumzia Yahwe kutawala mfalme kana kwamba mfalme alikuwa mnyama yahwe aliyetawala kwa lijamu na ndoano. "Nitakutawala kama mwanamume anavyotawala mnyama wake kwa ndoano katika pua yake na lijamu katika mdomo wake"

Nitakurudisha katika njia uliyotoka

Hii ina maana ya kusababisha mfalme kurudi katika nchi yake ya nyumbani. Maana ya hii inaweza kuwekwa wazi. "Nitakulazimisha kurudi katika nchi yako mwenyewe"

Isaiah 37:30

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza ujumbe wa Yahwe kwa Hezekia.

ishara kwako

"ishara kwako, Hezekia". Hapa "kwako" ni umoja na ina maana ya Hezekia.

utakula ... unapaswa kupanda

Hapa "utakula" ni wingi na ina maana ya watu wa Yuda.

mwaka wa pili

"mwaka wa pili"

katika mwaka wa pili kile kitakachoota

maneno ambayo hayapo yanaweza kuongezwa. "katika mwaka wa pili utakula kile kinachoota"

kile kitakachoota kutokana na hicho

"kile kitakachoota pori kutokana na hicho" au "kile kitakachoota pori"

Isaiah 37:31

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza ujumbe wa Yahwe kwa Hezekia.

waliobaki

"aliyesalia" ni sehemu ya kitu ambacho hubaki baada ya wengine kuondoka. Hapa ina maana ya watu ambao wamebaki Yuda.

nyumba ya Yuda

Hapa "nyumba" ya Yuda ina maana ya vizazi vyake. "vizazi vya Yuda"

atachipua tena mzizi na kuzaa matunda

Hii inazungumzia watu wa Yuda kuwa na mafanikio kana kwamba walikuwa mimea ambayo ingetoa mzizi na kuzaa matunda. "itafanikiwa kama mmea ambao huota mzizi na kuzaa matunda"

Kwa maana kutoka Yerusalemu aliyesalia atajitokeza; kutoka Mlima Sayuni waliokoka watakuja

Misemo hii miwili ina maana moja na inatumika pamoja kusisitiza watu waliosalia ambao waliokoka.

Ari ya Yahwe wa majeshi itafanya hivi

Hii inazungumzia Yahwe kufanya kitu kwa sababu ya ari yake kana kwamba "ari" yake ilikuwa ikifanya tendo kihalisia. "Kwa sababu ya ari yake, Yahwe wa majeshi atafanya hivi" au "Yahwe wa majeshi atafanya hivi kwa sababu ya ari yake"

Isaiah 37:33

Hatakuja ... Wala hatakuja

Hapa mfalme wa Ashuru anamaanisha wote yeye na jeshi lake. "Jeshi lake halitakuja ... Wala hawatakuja"

kwa ngao

"kwa ngao"

tuta la kuzingira

kilima kikubwa cha mchanga kilichojengwa dhidi ya ukuta wa mji ambacho huwezesha jeshi kushambulia mji

alikuja ... hataingia

Hapa mfalme wa Ashuru anamaanisha wote yeye na jeshi lake. "walikuja .. hawataingia"

Hili ni tamko la Yahwe

Hii inaweza kuandikwa ili kwamba nomino dhahania "tamko" lielezwa kama kitenzi "tamka" au "sema kwa dhati". "hivi ndivyo Yahwe wa majeshi alivyotamka" au "hivi ndivyo kile Yahwe wa majeshi alivyosema kwa dhati"

Isaiah 37:35

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza

kwa ajili ya

"kwa sababu"

Isaiah 37:36

kuwaua

Hii lahaja ina maana ya kua. "kuua"

Senakeribu mfalme wa Ashuru aliondoka Israeli na kwenda nyumbani na kukaa Ninawi

Hapa Senakeribu ina maana ya wote yeye na jeshi lake. Wote aliondoka Israeli na kurudi nyumbni Ashuru. Senakeribu alirudi katika mji wa Ninawi. "Senakeribu na jeshi lake aliondoka Israeli na kwenda nyumbani, na Senakeribu alibaki Ninawi"

Senakeribu

Hili ni jina la mfalme wa Ashuru.

Isaiah 37:38

alipokuwa akiabudu

"Senakeribu alipokuwa akiabudu"

Nsiroki

Hili ni jina la mungu wa uongo.

Adrameleki ... Shareza ... Esar-hadoni

Haya ni majina ya wanamume.

kwa upanga

"kwa panga zao"

Isaiah 38

Isaiah 38:1

Upange nyumba yako vizuri

Hii ina maana ya kuandaa familia yako na wale wanaosimamia masuala yako ili kwamba wajue cha kufanya baada ya kufa. Hii inaweza kuandikwa wazi. "Unatakiwa kuwaambia watu katika kasri kile unachotaka wao kufanya baada ya kufa"

weka akilini

Lahaja hii ina maana ya kukumbuka "kumbuka"

nilitembea kwa uaminifu mbele yako

Hii ni lahaja. Hapa "kutembea" ina maana ya "kuishi". Msemo una maana ya kuishi kwa njia ambayo inampendeza Yahwe. "aliishi kwa uaminifu mbele yako" au "alikutumikia kwa uaminifu"

kwa moyo wangu wote

Hapa "moyo" una maana ya undani wa mtu ambayo inawakilisha mtu kuwa na mapenzi ya dhati. "kwa utu wangu wote wa ndani" au "kwa mapenzi yangu yote"

kilichokuwa chema machoni pako

Msemo huu "machoni pako" ina maana ya kile Yahwe anachofikiri. "kile kinachokupendeza" au "kile unachokichukulia kuwa kizuri"

Isaiah 38:4

neno la Yahwe likaja

Hii ni lahaja ambayo inatumiwa kutambulisha kitu ambacho Mungu alimwambia manabii wake au watu wake. "Yahwe alizungumza ujumbe huu" au "Yahwe alizungumza maneno haya"

Tazama

Hii ni lahaja. Inatumika kuuliza wasikilizaji kuzingatia kwa makini kwa kile kinachosemwa. "Sikiliza"

miaka kumi na tano

"miaka 15"

mkono wa mfalme wa Ashuru

Hapa "mkono" wa mfalme una maana ya nguvu yake. "nguvu ya mflame wa Ashuru"

Isaiah 38:7

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na Hezekia.

Tazama

Hii ni lahaja. Yahwe anatumia neno hili kuvuta wasikilizaji kwa kile kinachosemwa baadaye.

ngazi za Ahazi

Ngazi hizi zina maana ya njia hii kwa sababu zilijengwa wakati Ahazi alikuwa mfalme.

Isaiah 38:9

hivyo katikati mwa maisha yangu

"ya kuwa kabla sijawa mzee". Hii ina maana ya kufa katika umri wa kati, kabla ya kuzeeka.

Nitapita katikati ya malango ya kuzimu

Hii inazungumzia kufa kana kwamba kuzimu ilikuwa ufalme ambao una malango ambayo mtu huingia. "Nitakufa na kuelekea kuzimu"

Nimetumwa kule kwa miaka yangu iliyobaki

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "kabla sijaishi miaka yangu yote nitaenda kaburini"

katika nchi ya wanaoishi

"Wanaoishi" ina maana ya watu ambao wapo hai" au "katika dunia hii ambamo watu wapo hai"

Isaiah 38:12

Maelezo yaJumla

Hezekia anaendelea maombi yake ya maandishi.

Maisha yangu yameondolewa na kubebwa mbali na mimi kama hema la mchungaji

Hii inazungumzia jinsi Yahwe anamaliza uhai wa Hezekia kwa haraka kwa kulinganisha kwa jinsi mchungaji anavyotoa hema lake kutoka ardhini. "Yahwe amechukua uhai wangu kutoka kwangu haraka kama mchungaji anavyopanga hema lake na kulibeba mbali"

Maisha yangu yameondolewa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe amechukua uhai wangu"

Nimekunjua maisha yangu kama mfumaji; unanikata kutoka katika kitanda cha mfumi

Hii inazungumzia Yahwe kumaliza uhai wa Hezekia haraka kwa kulinganisha na jinsi mfumaji hukata nguo yake kutoka katika kitanda cha mfumi na kukikunjua juu. "unamaliza uhai wangu haraka, kama mfumaji anavyokata nguo yake kutoka katika kitnda inapokamilika"

unakata

Hapa "unakata" ni umoja na ina maana ya Mungu.

kitanda cha mfumi

chombo kinachotumika kufuma uzi pamoja kutengeneza nguo.

kama simba anavunja mifupa yangu yote

Hezekia anazungumza jinsi alivyo katika maumivu makala kwa kulinganisha kuwa na mwili wake kuraruriwa na simba. "maumivu yangu ni kana kwamba nimeraruliwa na simba"

Isaiah 38:14

Maelezo ya Jumla

Hezekia anaendelea maombi yake ya maandishi.

Kama mbayuwayu ninalia; ninalia polepole kama njiwa

Vishazi hivi vyote viwili vina maana moja na vinasisitiza jinsi milio ya huzuni na kusikitisha ya Hezekia ilivyokuwa. Mbayuwayu na njiwa ni aina ya ndege. "Milio yangu ni ya kusikitisha - inasikika kama mlio wa mbayuwayu na sauti kama ya njiwa"

macho yangu

Hapa Hezekia ana maana ya yeye mwenyewe. "macho" yake yanasisitiza ya kwamba anatafuta kitu.

kwa kutazama juu

Hii ina maana ya Hezekia kutazama mbinguni kwa ajili ya Mungu kumsaidia. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "kwa kusubiri msaada unaokuja kutoka mbinguni" au "kwa kusubiri kwa ajili yako kunisaidia"

Ninaonewa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "ugonjwa wangu unanitesa mimi"

Niseme nini?

Hezekia anatumia swali kusisitiza hana chochote cha kusema. "Sina chochote kilichobaki cha kusema"

Nitatembea polepole

Hii ni lahaja. Hapa "kutembea" ina maana ya kuishi. "Nitatembea kwa unyenyekevu"

miaka yangu yote

Hii ina maana ya maisha yake yote yaliyobaka. "maisha yangu yaliyobaki"

kwa sababu nimezidiwa na majonzi

"kwa sababu nimejaa majonzi" au "kwa sababu nina huzuni sana"

Isaiah 38:16

Maelezo ya Jumla

Hezekia anaendelea maombi yake ya maandishi.

na maisha yangu yarudishwe kwangu

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "na unipatiea uhai wangu kwangu"

kutoka katika shimo la uharibifu

Hezekia hakufa lakini alikuwa karibu ya kufa. Hii ina maana Yahwe kumuokoa katika kufa. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "kutoka katika kifo na kwenda katika shimo la uharibifu" au "ili kwamba nisiweze kufa"

kwa kuwa umezitupa dhambi zangu nyuma ya mgongo wako

Hezekia anazungumzia Yahwe kusamehe dhambi zake kana kwamba zilikuwa vitu ambavyo Yahwe alitupa nyuma yake na kuvisahau. "kwa maana umesahau dhambi zangu zote na hauvifikirii tena"

Isaiah 38:18

Maelezo ya Jumla

Hezekia anaendelea maombi yake ya maandishi.

Kwa maana kuzimu haikushukuru wewe; kifo haikusifu wewe

Hapa "kuzimu" na "kifo" ina maana ya "watu waliokufa". "Kwa wale walio Kuzimu hawakushukuru; watu waliokufa hawakusifu"

wale waendao chini shimoni

"wale ambao hushuka katika kaburi"

hawatumaini katika uaminifu wako

"usiwe na matumaini katika uaminifu wako". Hapa "wako" ni umoja na ina maana ya Yahwe.

Mtu anayeishi, mtu anayeishi

Hezekia anarudia msemo huu kusisitiza ya kuwa mtu hai pekee, na sio mfu, anaweza kutoa shukurani kwa Yahwe.

Isaiah 38:20

Maelezo ya Jumla

Hezekia anaendelea maombi yake ya maandishi.

niokoe

Hii ina maana ya kuokolewa kutoka katika kufa. Inawez akuwekwa wazi zaidi. "niokoe katika kufa"

tutashangilia

Hapa "tutashangilia" ina maana ya Hezekia na watu wa Yuda.

Isaiah 38:21

Sasa

Neno hili linatumika kuweka alama ya pumziko katika simulizi kuu. Hii inatoa taarifa ya nyuma kuhusu Isaya na Hezekia.

Na wachukue

"Na watumishi wa Hezekia"

bonge la tini

Hii ilitumika kama lihamu. Maana inaweza kuwekwa wazi. "tumia lihamu ya tini ya kupondwa"

kuchemsha

eneo linalouma juu ya ngozi ambayo imeathirika

Isaiah 39

Isaiah 39:1

Merodaki-Baladani ... Baladani

Haya ni majina ya wanamume.

Hezekia alifurahiswah na mambo haya

Hii inaweza kuwekwa wazi zaidi. "Wajumbe wa mfalme walipofika, Hezekia alifurahishwa na kile walicholeta kwake"

aliwaonywesha wajumbe ghala yake yenye vitu vya thamani

"aliwaonyesha wajumbe kila kitu cha thamaniu alichokuwa nacho"

ghala

jengo ambapo bidhaa hukaa

kila kilichopatina ndani ya ghala yake

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "kila kitu ambacho kilikuwa ndani ya ghala zake"

Hapakuwa na kitu katika nyumba yake, wala katika ufalme wake, ambacho Hezekia hakuwaonyesha

Huku ni kukuza kidogo maana Hezekia aliwaonyesha vitu vingi, lakini sio kila kitu. Pia, hii inaweza kuelezwa kwa chanya. "Hezekia aliwaonyesha karibu kila kitu ndani ya nyumba yake na ndani ya ufalme wake"

Isaiah 39:3

Wameona kila kitu ndani ya nyumba yangu. Hakuna kitu miongoniu mwa vitu vyangu vya thamani ambacho sijawaonyesha

Sentensi hizi mbili zina maana moja na hutumika pamoja kusisitiza jinsi gani Hezekia aliwaonyesha wanamume.

kila kitu ndani ya nyumba yangu

Huku ni kukuza kidogo maana Hezekia aliwaonyesha vitu vingi, lakini sio kila kitu. "karibu ya kila kitu katika nyumba yangu"

Hakuna kitu miongoniu mwa vitu vyangu vya thamani ambacho sijawaonyesha

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya chanya. "Niliwaonyesha vitu vyangu vyote vya thamani katika kasri yangu"

Isaiah 39:5

Yahwe wa majeshi

Hili ni jina la Mungu wa watu wa Israeli.

neno

"ujumbe"

Tazama

Neno hili linatumika hapa kama lahaja kuvuta usikivu wa Hezekia kwa kile kinachofuatwa kusemwa. "Sikilizeni"

ambapo kila kitu katika kasri yako ... kitabebwa mpaka Babeli

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya chanya. "pale ambapo jeshi la adui litachukua kila kitu katika kasri yako ... kurudi Babeli"

Isaiah 39:7

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza ujumbe wa Yahwe kwa Hezekia.

wana watakaozaliwa kwako

"wana wako"

watawachukua

"Wababeli watawachukua"

Isaiah 40

Isaiah 40:1

Fariji, fariji

Neno "fariji" linarudwa kwa ajili ya msisitizo

asema Mungu wako

Hapa "wako" ni wingi na ina maana ya wale ambao nabii anawaambia kufariji watu wa Mungu.

Zungumza kwa upole kwa Yerusalemu

Nabii anazungumzia Yerusalemu kana kwamba ilikuwa mwanamke ambaye Yahwe alimsamehe. Kwa hiyo, Yerusalemu inawakilisha watu wanaoishi katika mji huo. Zungumza kwa upole kwa watu wa Yerusalemu"

tamka kwake ...ustawi wake ... udhalimu wake amepokea ... dhambi zake

Viwakilishi nomino vina maana ya Yerusalemu lakini inaweza kubadilishwa kama "watu wa Yerusalemu" inaazimwa kama tafsiri. "tangaza kwao ... ustawi wao ... udhalimu wao ... wamepokea ... dhambi zao"

ustawi wake

Maana zaweza kuwa ya kwamba neno "ustawi" lina maana ya 1) kwa vita ya kijeshi au 2) kwa kazi ya kulazimishwa.

udhalimu wake umesamehewa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe amesamehe udhalimu wake"

kutoka mkononi mwa Yahwe

Hapa neno "mkono" inawakilisha Yahwe mwenyewe. "kutoka kwa Yahwe"

Isaiah 40:3

Sauti inalia

Neno "sauti" inawakilisha mtu ambaye analia. "Mtu analia"

Katika nyika andaa njia ya Yahwe; weka wima katika Araba njia kwa ajili Mungu wetu

Mistari hii miwili ni sambamba na ina maana moja. Watu kujiandaa kwa ajili ya msaada wa Yahwe inazungumziwa kana kwamba walikuwa wakiandaa njia kwa ajili ya Yahwe kusafiri juu yake.

Araba

Hili ni jangwa.

Kila bonde litainuliwa juu, na kila mlima na kilima kitasawazishwa

Misemo hii inaelezea jinsi watu wanapaswa kuandaa njia kwa ajili ya Yahwe. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Inua juu kila bonde, na sawazisha kila mlima na kilima"

Kila bonde litainuliwa juu

Kufanya mabonde kuwa sawasawa na ardhi iliyobakiai inazungumziwa kana kwamba ilikuwa kuinua juu mabonde. "Kila bonde litajazwa"

na utukufu wa Yahwe utafunuliwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "na Yahwe atafunua utukufu wake"

kwa maana mdomo wa Yahwe umenena

Neno "mdomo" unawakilisha Yahwe mwenyewe. " kwa maana Yahwe umeizungumza"

Isaiah 40:6

Nyama yote ni nyasi

Neno "nyama" lina maana ya watu. Msemaji anazungumza kuhusu wanadamu kana kwamba ni nyasi, kwa sababu wote hufa haraka. "Watu wote ni kama nyasi"

agano lao la uaminifu ni kama maua ya shambani

Msemaji analinganisha agano la uaminifu la watu kwa maua ambayo huchanua na kisha kufa haraka. "agano lao la uaminifu lote huisha haraka, kama ua wa shamba liinavyokufa haraka"

uaminifu wa agano

Maana zaweza kuwa 1) agano la uaminifu au 2) uzuri.

pumzi ya Yahwe itakapopuliza juu yake

Maana zaweza kuwa 1) "Yahwe atakapopuliza pumzi yake juu yake" au 2) "Yahwe atakapotuma upepo kupuliza juu yake".

ubinadamu ni nyasi

Msemaji anazungumzia wanadamu kana kwamba ni nyasi, kwa sababu wote hufa haraka. "watu hufa haraka kama nyasi"

neno la Mungu wetu litasimama milele

Msemaji anazungumza kile Mungu anasema kudumu milele kana kwamba neno lake husimama milele. "vitu ambavyo Mungu wetu wanasema vitadumu milele"

Isaiah 40:9

Panda katika mlima wa juu, Sayuni, mletaji wa habari njema

Mwandishi anazungumzia Sayuni kana kwamba ilikuwa mjumbe anayetmka habari njema kutoka katika kilele cha mlima.

Panda katika mlima wa juu

Wajumbe mara kwa mara husimama juu ya nchi iliyoinuka, kama vile milima, ili kwamba watu wengi waweze kusikia kile walichotangaza.

Sayuni

Hii ina maana ya watu ambao wanaishi Sayuni. "nyie watu wa Sayuni"

Yerusalemu. Wewe uletaye habari njema

Mwandishi anazungumzia Yerusalemu kana kwamba ilikuwa mjumbe ambaye hutangaza habari njema.

na mkono wake wa nguvu hutawala kwa ajili yake

Hapa neno "mkono" linawakilisha nguvu ya Mungu. "na anatawala kwa nguvu kubwa"

dhawabu yake ipo pamoja naye ... wale ambao amewaokoa huenda mbele zake

Misemo hii miwili ina maana moja. Wale ambao aliwaokoa ni "zawadi" yake. "anawaleta wale aliowaokoa pamoja naye kama zawadi yake"

Isaiah 40:11

Atalisha kundi lake kama mchungaji

Mwandishi anazungumzia watu wa Yahwe kana kwamba walikuwa kondoo na juu ya Yahwe kana kwamba alikuwa mchungaji wao. "Atawatunza watu wake kama mchungaji anavyolisha kundi lake"

Isaiah 40:12

Ambaye amepima ... au vilima juu ya mizani?

Maswali haya ya balagha yanatarajia jibu la kukana na linasisitiza ya kwamba ni Yahwe pekee anaweza kufanya vitu hivi. "Hakuna mwingine ila Yahwe amepima ... na vilima katika mizani".

aliyepima maji katika uwazi wa mkono wake

Yahwe kujua wingi wa maji uliomo katika bahari inazungumziwa kana kwamba Yahwe alishika maji katika mkono wake.

aliyepima anga kwa upana wa mkono wake

"upana" ni kipimo cha urefu katikati ya kidole gumba n kidole kidogo mkono unaponywoshwa. Yahwe kujua urefu wa anga inazungumziwa kana kwamba alipima kwa mkono wake.

aliyeshika vumbi la dunia katika kikapu

Yahwe kujua wingi wa vumbi ulivyo katika dunia inazungumziwa kana kwamba alilibeba katika kikapu.

aliyepima uzito wa milima katika mizani, au vilima katika mizani?

Yahwe kujua jinsi milima iilivyo mizito inazungumziwa kana kwamba alipiima kwa mizani.

Isaiah 40:13

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kutumia maswali kusisitiza utofauti wa Yahwe.

Ni nani ameelewa akili ya Yahwe, au kumwelekeza kama mshauri wake?

Swali hili la balagha linatarajia jibu la kukana na kusisitiza ya kwamba hakuna mtu aliyewahi kufanya vitu hivi. "Hakuna mtu aliyeelewa akili ya Yahwe, na hakuna mtu alimwelekeza kama mshauri wake".

ameelewa akili ya Yahwe

Hapa neno "akili" lina maana ya mawazo ya Yahwe, lakini pia na hamu na motisha zake.

Kutoka kwa nani alwahi kupokea maelekezo?

Swali hili la balagha linatarajia jibu la kukana na linasisitiza ya kwamba hakuna mtu aliyewahi kufanya hivi. "Hajawahi pokea maelekezo kutoka kwa mtu"

Nani alimfundisha njia sahihi ya kufanya mambo, na kumfundisha uelewa, au kumwonyesha njia ya maarifa?

Swali hili la balagha linatarajia jibu la kukana na kusisitiza ya kwamba hakuna mtu aliyewahi kufanya vitu hivi. "Hakuna mtu aliyemfundisha njia sahihi ya kufanya vitu. Hakuna mtu aliyemfundisha uelewa. Hakuna mtu aliyemwonyesha njia ya maarifa".

Isaiah 40:15

Tazama ... angalia

Maneno haya huongeza msisitizo kwa kile kinachofuata.

mataifa ni kama tone katika ndoo, na yanachukuliwa kama vumbi katika mizani

Nabii analinganisha mataifa kwa tone la maji na kwa vumbi ili kusisitiza jinsi yalivyo madogo na kutokuwa na umuhimu kwa Yahwe.

kama tone katika ndoo

Maana zaweza kuwa 1) tone la maji ambalo huanguka katika ndoo au 2) tone la maji ambalo hudondok nje ya ndoo.

na wanachukuliwa kama vumbi katika mizani

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "na Yahwe anawachukulia kama vumbi juu ya mizani"

yanachukuliwa na yeye kama si kitu

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "anayachukulia kutokuwa kitu"

Isaiah 40:18

Mtamlinganisha Mungu na nani? Kwa sanamu ipi mtamfananisha naye"

Isaya anatumia maswali mawili ya kufanana kusisitiza ya kwamba hakuna sanamu ambayo inaweza kufanana na Mungu. "Hakuna mtu ambaye unaweza kulinganisha na Mungu. Hakuna sanamu ambayo unaweza kumfananisha"

utamfananisha

Huu ni wingi na ina maana ya watu wote wa Mungu.

Fundistadi huichonga: sonara anavyoifunika kwa hahabu na kuichonga mikufu ya fedha kwa ajili yake

"Mtumishi mwenye ujuzi huiunda, mwingine huifunika kwa dhahabu, na kutengeneza mkufu wa fedha kwa ajili yake"

Isaiah 40:21

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza na watu wa Mungu.

Je! haujajua? Haujasikia? Haijaambiwa kwako toka mwanzo? Haujaelewa toka misingi ya dunia?

Isaya anatumia maswali haya kusisitiza ya kwamba watu wanapaswa kujua ukuu wa Yahwe kma muumba. "Kwa uhakika unajua na umesikia! Imeambiwa kwako toka mwanzo; umeelewa toka misingi ya dunia!"

Haijaambiwa kwako toka mwanzo?

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Je! watu hawajakuambia toka mwanzo?"

toka misingi ya dunia

Nabii anazungumzia Yahwe kuumba dunia kana kwamba dunia ilikuwa jengo ambalo Yahwe alilaza msingi. "kutoka kipindi ambacho Yahwe aliumba dunia"

Yeye ndiye ambaye hukaa juu ya upeo wa macho ya dunia

Nabii anazungumzia Yahwe kutawala dunia kana kwamba Yahwe alikuwa amekaa juu ya kiti cha enzi juu ya dunia.

wakazi ni kama panzi mbele zake

Nabii analinganisha namna ambavyo Yahwe anachukulia wanadamu kwa namna ambavyo wanadamu wangechukulia panzi. Kama vile panzi ni wadogo kwa binadamu, binadamu ni wadogo na dhaifu mbele za Mungu.

Ananyosha mbingu kama pazia na kuitawanya kama hema la kuishi ndani

Mistari hii miwili inatumia maana ya kufanana. Nabii anazungumzia Yahwe kuumba mbingu kana kwamba alisimamisha hema ambalo ataishi. "Anatawanya mbingu kwa urahisi kama mtu anavyonyosha pazia au kusimamisha hema ambalo anishi"

Isaiah 40:23

Hupunguza

"Yahwe hupunguza"

Tazama ... tazama ... tazama

Maneno haya yanaongeza msisitizo kwa kinachofuata.

wamepandwa muda si mrefu ... nao wananyauka

Nabii anazungumzia watawala kutojiweza mbele ya Yahwe kana kwamba walikuwa mimea mipya ambayo hunyauka pale upepo wa moto hupuliza juu yao.

wamepandwa muda si mrefu ... wameoteshwa muda si mrefu

Misemo hii miwili ina maana moja na inamaansha lengo ambalo mimea au mbegu inawekwa katika ardhi. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "baada tu ya mtu kuipanda ... baada tu ya mtu kusia"

anapuliza juu yao

Nabii anazungumzia Yahwe kuondoa watawala kutoka kwenye madaraka kana kwamba Yahwe alikuwa upepo unaochoma juu ya mimea na kusababisha inyeuke.

upepo unawapuliza kama majani makavu

Tashbihi hii inaongeza sitiari ya watawala kuwa mimea na Yahwe kama upepo ambao husababisha wao kunyauka. Hukumu ya upepo wa Yahwe utaondoa mimea iliyonyauka kirahisi kama upepo unavyopuliza majani makavu.

Isaiah 40:25

Ni kwa nani utanilinganisha mimi, ni nani nayefanana naye?

Yahwe anatumia maswali mawili ya kufanana ya balagha kusisitiza ya kuwa hakuna mtu kama yeye. "Hakuna mtu ambaye unaweza kulinganisha na mimi. Hakuna mtu ambaye ninamfanana".

Nani ameumba nyota hizi zote?

Hili ni swali la kufokeza ambalo linaashiria jibu, Yahwe. "Yahwe ameziumba nyota hizi zote!"

Yeye huongoza mpangilio wao

Hapa neno "mpangilio" una maana ya mpangilio wa kijeshi. Nabii anazungumzia nyota kana kwamba zilikuwa wanajeshi ambao Yahwe huamuru kujitokeza.

Kwa ukuu wa uwezo wake na kwa wingi wa nguvu zake

Misemo "ukuu wa uwezo wake" na "wingi wa nguvu zake" huunda mambo mawili ambayo husisitiza uweza wa Yahwe. "Kwa uwezo wake mkubwa na wingi wa nguvu"

hakuna mmoja asiyeonekana

Kauli hii ya kukana inasisitiza jambo chanya. "kila mmoja yupo"

Isaiah 40:27

Kwa nini unasema, Yakobo, na kutamka, Israeli ... uthibitisho"?

Swali linasisitiza ya kwamba hawatakiwi kusema wanachosema. "Hautakiwi kusema, enyi watu wa Israeli ... uthibitiisho'".

Kwa nini unasema, Yakobo, na kutamka, Israeli

Misemo hii miwili yote ina maana ya watu wa Israeli. "Kwa nini unasema, enyi watu wa Israeli"

Njia yangu imefichwa kutoka kwa Yahwe

Yahwe kutojua kinachotokea kwao inazungumziwa kana kwamba Yahwe hakuweza kuona njia ambayo ninasafiria. "Yahwe hajui kinatoke kwangu"

Mungu wangu hajihusishi juu ya uthibitisho wangu

Maana zaweza kuwa 1) "Mungu wangu hajihusishi juu ya wengine kunitendea kinyume n haki" au 2) "Mungu wangu hajihusishii juu kunitendea haki".

Je! haujajua? Haujasikia?

Isaya anatumia maswali haya kusisitiza ya kwamba watu wanatakiwaa kuja ukuu wa Yahwe. "Hakika unafahamu na umesikia!"

mwisho wa dunia

Sehemu katika dunia ambazo zipo mbali sana zinazungumziwa kana kwamba zilikuwa sehemu ambapo dunia huwa mwisho. Msemo huu pia huunda neno moja kwa ajilii ya maneno mengiine kumaanisha kila sehemu katikati ya hizi mwisho. "sehemu za mbali za dunia" au "dunia nzima"

Isaiah 40:29

Hutoa nguvu kwa waliochoka; na kwa wadhaifu hutoa nguvu mpya

Mistari hii miwili inatuma maana za kufanana na husisitiza ya kwamba Yahwe hutia nguvu wale ambao hawana nguvu.

Hutoa nguvu

"Yahwe hutoa nguvu"

watapaa kwa mabawa kama tai

Watu kupokea nguvu kutoka kwa Yahwe inazungumziwa kana kwamba watu waliweza kupaa kama tai wanavyopaa. Tai ni ndege ambaye hutumiwa mara kwa mara kama alama ya uwezo na nguvu.

watakimbia na kuwatachoka; watatembea na hawazimia

Mistari hii miwili inatumia maana za kufanana. Watu kupata nguvu kutoka kwa Yahwe inazungumziwa kana kwamba waliweza kukimbia na kutembea bila kuchoka.

Isaiah 41

Isaiah 41:1

Sikiliza mbele zangu kwa utulivu

Hapa "zangu" ina maana ya Mungu.

enyi nchi za pwani

Hii ina maana ya watu ambao huishi katika visiwa na katika nchi zinazopatikana au ng'ambo ya pili ya Bahari ya Mediteranea.

wafanye upya nguvu zao

Yahwe hutia nguvu wale ambao hawana nguvu.

waache waje karibu na kuongea; tuache tukaribie pamoja kuamua mabishano

Misemo hii miwili hutumia maana moja. Msemo wa pili unafafanua sababu kwa ajili ya kwanza. "waache waje karibu ili wawvze kuzungumza na kuamua pamoja nami"

Ni nani aliyemwamsha yule kutoka mashariki, kumwita katika haki kwa huduma yake?

Yahwe anatumia swali hili kusisitiza ya kwamba yeye ndiye aliyesababisha mtawala huyu kutoka mashariki kuwa mshindi. "Mimi ndiye niliyemwita mtawala huyu wa nguvu kutoka mashariki na kumweka katika huduma nzuri"

Hukabidhi mataifa kwake

"Ninawapa mataifa kwake" au "Yule anayefanya mambo haya hukabidhi mataifa kwake"

Huyageuza kwa vumbi kwa upanga wake, kama mashina ya mabua yalipulizwa kwa upepo kwa upinde wake

Mataifa ambaye yule wa mashariki yanalinganshwa kwa vumbi na mashina ya mabua, kwa sababu yote yatakuwa madogo sana kama vitu hivi na kwa sababu jeshi lake litayasambaza kirahisi.

Isaiah 41:3

Taarif ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza kwa nchi za pwani na mataifa

Huwafuatilia na kuwapita kwa usalama

"Mtawala kutoka mashariki hufuatilia mataifa"

kwa njia nyepesi ambayo miguu yake hugusa kwa nadra

Maana zaweza kuwa 1) hii ni sitiari ambayo yeye na jeshi lake kusogea haraka sana inazungumziwa kana kwamba miguu yake hugusa ardhii kwa nadra. "kwa njia ambayo anasogea kwa kasi kubwa" au 2) "miguu" ni sawa na msemo unaodokeza ya kuwa hii ni njia ambayo wamesafiri hapo awali. "kwa njia ambayo hajawahi kusafiria kabla"

Ni nani ametenda na kutimiza mambo haya?

Yahwe anatumia swali hili kusisitiza ya kwamba yeye ndiye ambaye amefanya mambo haya. "Nimefanya na kutimiza mambo haya"

Ni nani aliyeita vizazi kutoka mwanzo?

Hapa neno "vizazi" linawakiliisha wanadamu wote, ambao Yahwe aliwaumba na kuwaongoza katika historia. Swali la balagha linatarajia jibu, Yahwe. "Nimewaita vizazi vya wanadamu kutoka mwanzo"

ametenda na kutimiza

Maneno haya mawili yana maana moja na husisitiza ya kwamba Yahwe ndiye aliyefanya mambo haya.

wa kwanza, na wale wa mwisho

Maana zaweza kuwa 1) ya kuwa Yahwe alikuwepo kabla ya uumbaji na atakuwepo katika mwisho wa uumbaji au 2) ya kuwa Yahwe alikuwepo kabla ya kizazi cha kwanza ya wanadamu na atakuwepo katika kizazi cha mwisho cha wanadamu.

Isaiah 41:5

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza.

Visiwa hivi ... mwisho wa dunia

Misemo hii inawakilisha watu ambao wanaishi maeneo hayo. "Watu ambao huishi katika vsiwa ... watu ambao huishi katika mwisho wa dunia"

Visiwa

Hii ina maana ya watu ambao huishi katika visiwa na katika nchi zinazopatikana au ng'ambo ya pili ya Bahari ya Mediteranea.

mwisho wa dunia

Sehemu katika dunia ambazo zipo mbali sana na zinazungumziwa kana kwamba ni sehemu ambapo dunia huwa mwisho. "sehemu za mbali za dunia"

vinakaribia na kuja

Hizi mbili zina maana ya kwamba watu hujikusanya pamoja. "wanakuja pamoja"

fuawe

kipande cha chuma ambacho mtu kuchonga chuma kwa nyundo

kusema juu ya kuchomelea

Hapa neno "kuchomelea" lina maana ya njia ya kukaza dhahabu kwa mbao pale ambapo watumishi humaliza kutengeneza sanamu.

Wanaikaza kwa misumari ili kwamba isianguke

Hapa "isianguke" ina maana ya sanamu ambayo walitengeneza.

Isaiah 41:8

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza.

wewe ambaye ninakurudisha kutoka katika mwsho wa dunia, na ambaye nilimwita kutoka sehemu za mbali

Mistari hii miwili ina maana moja na inasisitiza ya kwamba Yahwe analeta watu wa Israeli kutoka katika nch kutoka nchi za mbali.

mwisho wa dunia

Sehemu katika dunia ambazo zipo mbali sana na zinazungumziwa kana kwamba ni sehemu ambapo dunia huwa mwisho. "sehemu za mbali za dunia"

Nimekuchagua na sijakukataa

Misemo hii miwili ina maana moja. Wa pilii unaeleza katika maneno ya kukana kwa msemo wa kwanza unavyoeleza maneno ya chanya.

Isaiah 41:10

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Nitakuthibitisha kwa mkono wangu wa kuume wa haki

Yahwe kuimarisha watu wake inazungumziwa kana kwamba alikuwa akiwashikilia kwa mkono wake.

mkono wangu wa kuume wa haki

Hapa "mkono wa kuume" unawakilisha nguvu ya Yahwe. Maana zaweza kuwa 1) mkono wa kuume wa Yahwe ni wa haki yaani daima atafanya jambo sahihi. "nguvu yangu ya haki" au 2) mkono wa kuume wa Yahwe ni wa ushindi yaani atafanikiwa kwa kile anachofanya. "nguvu yangu ya ushindi"

Isaiah 41:11

Taarfa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

wataona haya na kuaibika, wote ambao walikuwa na hasira juu yako

"wote ambao walikuwa na hasira na wewe watapata haya na kuaibika"

wataona haya na kuaibika

Maneno haya mawili yana maana moja na husisitiza ukuu wa aibu yao.

watakuwa si kitu na kuangamia, wale wanaopingana na wewe

"wale ambao wanapingana na wewe watakuwa si kitu na wataangamia"

Isaiah 41:12

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Mimi ... nitashika mkono wako wa kiume

Yahwe kuwasaidia watu wa Israeli inazungumzwa kana kwamba alikuwa akishikilia mkono wao wa kulia.

Isaiah 41:14

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Yakobo wewe funza, na nyie watu wa Israeli

Hapa "Yakobo" na "watu wa Israeli" ina maana moja. "nyie watu wa Israeli ambao ni kama funza"

Yakobo wewe funza

Maana zaweza kuwa 1) ya kwamba ina maana ya mawazo ya mataifa mengine kuhusu watu wa Israeli au 2) ya kwamba hii ina maana ya mawazo ya Israeli wenyewe. Yahwe anazungumziwa umuhimu wao kana kwamba walikuwa funza.

tamko la Yahwe

Hii inaweza kuandikwa ili kwamba nomino dhahania "tamko" linaelezwa kama kitenzi "tamka" au "kusema kwa dhati". "Yahwe alitamka" au "Yahwe alisema kwa dhati"

Mtakatifu wa Israeli

Mtakatifu wa Israeli

Ninakufanya kama chombo cha kupura yenye ncha kali ... utaifanya vilima kuwa kama makapi

Yahwe anazungumzia kuwawezesha Israeli kuwashinda adui zao kana kwamba alikuwa akifanya taifa kuwa chombo cha kupura ambayo itasawazisha milima.

chombo cha kupura yenye ncha kali

chombo cha kupura ilikuwa ubao wenye uma zenye ncha kali ambazo mtu huvuta juu ya ngano kugawanyisha nafaka kutoka na makapi.

makali pande mbili

Hii ina maana ya pande za uma ambazo ziliungwa katika chombo cha kupura. Ya kwamba walikuwa "makali pande mbili" ina maana walikuwa na makali sana.

utapura milima na kuikanyaga

Badala ya kupura nafaka, Israeli atapura milima, ambayo inawakilisha mataifa yenye nguvu ambayo yalikuwa adui wa Israeli. "utapura adui zako na kuwaponda kana kwamba walikuwa nafaka, ingawa wanaonekana kuwa kama milima imara"

utaifanya vilima kuwa kama makapi

Mstari huu una maana sawa na mstari wa nyuma lakini unawakilisha hatua inayofuata katika njia ya kupura nafaka.

Isaiah 41:16

Kauli Kiunganishi

Yahwe anaendelea kutumia sitiari ya kugawanyisha nafaka kwa makapi kufafanua jinsi Israeli atakavyoshinda adui zake.

Utawapepeta ... upepo utawatawanya

Hapa neno "utawapepeta" ina maana ya milima na vilima katika 41:14. Hii inawakilisha hatua inayofuata katika njia ya kupura nafaka, ambapo nafaka hupepetwa kuondoa makapi. Adui wa Israeli watatoweka kama makapi yanayopulizwa kwa upepo.

upepo utawabeba mbali; upepo utawatawanya

Misemo hii miwili ina maana moja. "upepo utawapuliza mbali"

Isaiah 41:17

Taarifa ya Jumla

Yahwe anazungumzia watu ambao wapo katika mahitaji makubwa kana kwamba walikuwa na kiu kubwa sana, na utoaji wake kwao kana kwamba alisababisha maji kutokeza katka maeneo ambapo kwa kawaida hayatokei.

Isaiah 41:19

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza

mihadasi ... msonobari na miti ya mvinje

Hii ni aina ya miti

mkono wa Yahwe umefanya haya

Hapa neno "mkono" unawakilisha Yahwe mwenyewe. "Yahwe amefanya hivi"

Isaiah 41:21

Taarifa ya Jumla

Katika mistari hii, Yahwe anakejel watu na sanamu zao. Anazipa changamoto sanamu ziseme nini kitatokea katika siku za usoni, lakini anajua haziwezi.

Isaiah 41:23

Kauli Kiunganishi

Yahwe anaendelea kudhihaki sanamu na watu ambao huziabudu.

fanya kitu chema au kiovu

Maneno "chema" na "kiovu" huunda neno la maana moja na neno na linawakilisha kitu chochote. "fanya kitu chochote"

yule ambaye anakuchagua

Hapa "anakuchagua" ni wingi na ina maana ya sanamu. "mtu ambaye huchagua sanamu"

Isaiah 41:25

Taaarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza.

Nimemwinua juu mmoja

Yahwe anazungumzia kumteua mtu kana kwamba alimwinua mtu huyo juu. "Nimemteua mmoja"

kutoka katika kuchomoza kwa jua

Hii ina maana ya mashariki, upande ambapo jua linachomoza. "kutoka mashariki"

yeye anayeliita jina langu

Maana zaweza kuwa 1) ya kwamba mtu huyu humwomba Yahwe kwa ajili ya mafanikio yake au 2) ya kwamba mtu huyu humwabudu Yahwe.

atawakanyaga watawala

Kushinda watawala wa mataifa mengine inazungumziwa kana kwamba likuwa kuikanyaga chini ya miguu. "atawashinda watawala hawa"

kama mfinyanzi ambaye kuknyaga juu ya udongo

Yahwe analinganisha njia ambayo mtu huyu atakanyaga watawala wengine kwa njia ambayo mfinyanzi hukanyaga juu ya udongo kuchanganya kwa maji.

Ni nani aliyetangaza hili kutoka mwanzo, ili tuweze kujua? Kabla ya muda huu, ili tuweze kusema, "Yupo sahihi"?

Yahwe anatumia maswali haya ya balagha kudhihaki sanamu amabazo watu huabudu. Jibu linalodokezwa ni 1) ya kwamba sanamu hazijafanya mambo haya na 2) ya kwamba Yahwe ndiye ambaye alifanya mambo haya. "Hakuna kati ya sanamu ametangaza hiki kutoka mwanzo, ili tuweze kujua. Na hakuna kati yao aliyetangaza hili kabla ya wakati, ili tuweze kusema, "Yupo sahihi".

"Kweli, hakuna kati ya sanamu aliagiza hivyo. Kweli, hakuna mtu aliyesikia nyie sanamu mkisema chochote"

"Kweli, hakuna kati ya sanamu alagiza hivyo. Kweli, hakuna mtu aliyesikia nyie sanamu mkisema chochote"

Isaiah 41:27

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza.

hakuna mmoja kati yao

"hakuna sanamu moja"

viumbe vyao vya chuma vilivyochongwa ni upepo na utupu

Yahwe anazungumzia kutokuwa na thamani kwa sanamu kana kwamba sanamu ni upepo na si kitu kabisa. "sanamu zao hazina thamani"

Isaiah 42

Isaiah 42:1

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza

Tazama, mtumishi wangu

"Tazama, mtumishi wangu" au "Mtumishi wangu huyu hapa"

ndani yake ninafurahi

"ambaye ninayo furaha naye"

Isaiah 42:3

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza.

Tete lililopondwa hataivunja, na utambi unowaka kwa chini hatauzima

Yahwe anazungumzia watu dhaifu na wasiojiweza kana kwamba walipondwa kama matete na kuwaka kwa chini kama utambi.

Tete lililopondwa

Tete ni shina la mmea refu na jembamba kama nyasi ndefu. Kama likipondwa, haliwezi kubeba uzito wowote.

hataivunja

"Mtumishi wangu hatavunja"

nchi za pwani

Hii ina maana ya watu ambao huishi katika visiwa na katika nchi zenye mipaka au ng'ambo ya pili ya Mediteranea. "watu ambao wanaishi katika nchi za pwani"

Isaiah 42:5

yule aliyeziumba mbingu na kzitandaza, yule ambaye alitengeneza dunia

Nabii anazungumzia Yahwe kuziumba mbingu na dunia kana kwamba mbingu na dunia ilikuwa akitambaa ambacho Yahwe alizitandaza.

hutoa pumzi kwa watu juu yake na uzima kwa wale wanaoishi ndani yake

Misemo hii ina maana moja na inasisitiza ya kwamba Yahwe hutoa uhai kwa kila mtu. Neno "pumzi" ni neno kwa ajili ya uhai. "hutoa uhai kwa watu ambao wanaishi juu ya dunia"

nimekuita

Hapa "nimekuita" ni umoja na ina maana ya mtumishi wa Yahwe.

Nita ... kukutenda kama agano kwa ajili ya watu

Hapa neno "agano" ni neno kwa ajili ya yule anayeimarisha au patanisha agano. "Nita ... kukufanya kuwa mpatanishi wa agano kwa watu"

nuru kwa Mataifa

Yahwe anazungumzia kumfanya mtumishi wake yule ambaye atakomboa mataifa kutoka kifungoni kana kwamba alikuwa akimfanya nuru ambayo hung'aa katika maeneo ya giza kwa Mataifa.

Isaiah 42:7

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kufafanua kile mtumishi wake atafanya.

kufungua macho ya vipofu

Kusababisha watu vipofu kuona inazungumziwa kana kwamba ilikuwa kufungua macho yao. Pia, Yahwe anazungumzia mtumishi wake kuwaokoa wale ambao wamefungwa kimakosa kana kwamba mtumishi wke alikuwa akirejesha kuona kwa watu vipofu. "kuwezesha vipofu kuona"

kuwaacha huru wafungwa kutoka gerezani, na kutoka nyumba ya ulinzi mkali kwa wale wanaokaa gizani

Misemo hii miwili ina maana moja. Kitenzi kinaweza kutumka katika msemo wa pili. "kuwaacha huru wafungwa kutoka gerezani, na kuwaacha huru wale wanaokaa gizani kutoka nyumba ambayo wameshikiliwa"

Isaiah 42:8

wala sifa yangu pamoja na sanamu za kuchongwa

Kitenzi kinaweza kutumika kutoka msemo wa nyuma. "wala sitagawana sifa yangu na sanamu za kuchonga"

sifa yangu

Hii ina maana ya sifa ambayo Yahwe hupokea kutoka kwa watu.

nitakueleza

Hapa "nitakueleza" ni wingi na ina maana ya watu wa Israeli.

Isaiah 42:10

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza

bahari, na vyote vilivyomo, nchi za pwani, na wale wanaoishi pale

"na viumbe wote ambao huishi katika bahari, na wale wote wanaoishi katika nchi za pwani"

Acha jangwa na miji ipaze sauti

Hii ina maana ya watu wanaoishi katika jangwa na miji.

Kedari

Hili ni eneo kule Uarabuni. Kedari inawakilisha idadi ya watu wa Kedari. "ya watu wa Kedari"

Sela

wakazi wa Sela - Sela ni mji wa Edomu.

Isaiah 42:12

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza.

Waache watoe utukufu

Hapa "waache" ina maana ya watu katika nchi za pwani.

Yahwe atatoka nje kama hodari; kama mwanamume wa vita

Yahwe analinganishwa na hodari ambaye yupo tayari kuwashinda watu wa adui zake.

atamwamsha ari yake

Hapa "ari" ina maana ya uchu ambao hodari hupitia anapokaribia kupigana vita. Yahwe kuchangamsha ari yake inazungumziwa kana kwamba aliamsha kama upepo unapoamsha mawimbi ya maji.

Isaiah 42:14

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza.

Nimekaa kimya kwa muda mrefu; Nilikuwa nimetulia n kujizuia

Mistari hii miwili inagawana maana ya kufanana. Kutulia kwa Yahwe kunafafanuliwa kama ukimya na utulivi.

Nilikuwa nimetulia n kujizuia

Misemo hii miwili inagawana jambo moja na hudokeza ya kwamba Yahwe amejizuia kutotenda. "Nimejizuia kutofanya chochote"

Nitalia kama mwanamke katika uchungu; nitahema na kutweta

Utulivu wa Yahwe kama hodari anayepaza sauti inalinganishwa na mwanamke mwenye mimba anayelia kwa maumivu ya uchungu. Hii inasisitiza tendo la ghafla lisilozuilika baada ya kipindi cha utulivu.

Nitafanya milima kuwa takataka ... Nitakausha mabwawa

Yahwe anatumia lugha hii ya kisitiari kufafanua nguvu yake kubwa kushinda adui zake.

mabwawa

Bwawa ni eneo laini, lililo tepe tepe lenye madimbwi ya maji

Isaiah 42:16

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza.

Nitawaleta vipofu kwa njia ambayo hawajui; katika njia ambayo hawaijui nitawaongoza

Misemo hii miwili ina maana moja. "Nitawaongoza vipofu katika njia ambayo hawajui"

vipofu

Yahwe anazungumzia watu wake kutojiweza kana kwamba hawawezi kuona kwa sababu walikuwa vipofu.

ambayo hawaijui

Maana zaweza kuwa 1) "ya kwamba hawajawahi kusafiri" au 2) "ambayo hawana uzoefu nao"

Nitageuza giza kuwa nurur mbele yao

Yahwe anazungumzia watu wake kutojiweza kana kwamba hawakweza kuona kwa sababu walitembea gizani, na kusaidia kwake kana kwamba alisababisha mwanga kung'ara katika giza.

Isaiah 42:17

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza

Watageuzwa; watafedheheshwa kabisa

Kuwakataa wale ambao huabudu sanamu inazungumziwa kana kwamba ni kuwalazimisha kugeuka na kuelekea upande mwingine. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Nitawakataa na kuwatia aibu"

Isaiah 42:18

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza

wewe kiziwi ... wewe kipofu

Hapa "wewe" ni wingi na ina maana ya watu wa Israeli. Yahwe anazungumzia kushindwa kwao kumsikliza na kumtii kana kwamba walikuwa viziwi na vipofu.

Ni nani aliye kipofu ila mtumishi wangu? Au kiziwi kama mjumbe wangu nayemtuma?

Yahwe anauliza maswali haya ya balagha kukaripia watu wake na kusisitiza ya kwamba hakuna mtu aliye kipofu au kiziwi kama walivyo. "Hakuna mtu aliye kipofu kama mtumishi wangu. Hakuna mtu aliye kiziwi kama mjumbe wangu ambaye namtuma"

Ni nani aliye kipofu kama mwenzangu wa agano, au kipofu kama mtumishi wa Yahwe?

Yahwe anauliza maswali haya ya balagha kukaripia watu wake na kusisitiza ya kwamba hakuna mtu aliye kipofu au kiziwi kama walivyo. "Hakuna aliye kipofu kama mwenzangu wa agano. Hakuna aliye kipofu kama mtumishi wa Yahwe".

Isaiah 42:20

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza wtu wa Israeli.

Unaona mambo mengi, lakini hauelewi

"Ingawa unaona mambo mengi, hauelewi kile wanachomaanisha"

masikio yapo wazi, lakini hakuna anayesikia

Uwezo wa kusikia inazungumziwa kana kwamba masikio yalikuwa wazi. Hapa neno "kusikia" ina maana ya kuelewa kile mtu anachosikia. "watu husikia, lakini hakuna mtu anayeelewa kile wanachosikia".

Ilimpendeza Yahwe kusifu haki yake na kufanya sheria yake kutukuka

"Yahwe alifurahishwa kuinua haki yake kwa kufanya sheria zake kutukuka". Sehemu ya pili ya msemo huu unafafanu jinsi Yahwe ametimiza sehemu ya kwanza.

Isaiah 42:22

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza.

Lakini hawa ni watu walionyanganywa na kuporwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Lakini adui amenyanganya na kupora watu hawa"

walionyanganywa na kuporwa

Maneno haya mawili yana maana moja na husisitiza jinsi adui alivyowapora sana.

wote wametegwa ndani ya mashimo, kushikwa mateka ndani ya magereza

Misemo hii miwili ina maana moja. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "adui amewatega wote katika mashimo na kuwashika mateka katika magereza"

Isaiah 42:23

Taarifa ya Jumla

Hapa Isaya anaanza kuzungumza

Nani kati yenu

Hapa "yenu" ni wingi na ina maana watu wa Israeli.

Ni nani alimpatia Yakobo kwa mnyanganyi, na Israeli kwa waporaji?

Misemo hii miwili ina maana ya jambo moja. Isaya anatuma hii kama swali la kuongoza ili kusisitiza jibu ambalo atalitoa katika msemo unaofuata. "Nitakuambia ni nani aliwapa watu wa Israeli kwa wanyanganyi na waporaji"

Je! haikuwa Yahwe ... walikataa kutii?

Isaya anatumia swali hili la balagha kusisitiza ya kwamba Yahwe pekee alikuwa anawajibika kwa hali ya Israeli, na kufafanua sababu ambayo Yahwe alifanya vile. "Hakika alikuwa Yahwe ... walikataa kutii".

ambaye tumetenda dhambi dhidi yake

Hapa neno "tumetenda" ina maana ya watu wa Israeli na Isaya.

ambazo katika njia zake walikataa kutembea, na katika sheria yake walikataa kutii

Neno "walikataa" pia ina maana ya watu wa Israeli na Isaya. Misemo miwili ina maana moja. Katika ya kwanza, kutii sheria za Yahwe inazungumziwa kana kwamba ilikuwa kutembea katika njia ambayo Yahwe aliamuru kutembea.

Isaiah 42:25

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza

Kwa hiyo ali

"Kwa hiyo Yahwe"

alimwaga ghadhabu yake kali dhidi yao

Isaya anazungumzia ghadhabu ya Yahwe kana kwamba ilikuwa kimiminikio ambacho kinaweza kumwagwa nje. "alionyesha ghadhabu yake kali kuwaelekea wao"

dhidi yao

"dhidi yetu". Hapa "yao" ina maana ya watu wa Israelii, lakini Isaya bado anajumlisha mwenyewe kama sehemu ya watu.

kwa uharibifu wa vita

Neno "uharibifu" linaweza kutafsiriwa kwa kitenzi. "kwa kuwaharibu wao kwa vita"

Uliwaka kuwazunguka ... ukawaunguza

Isaya anazungumzia ghadhabu kali ya Yahwe kana kwamba ilikuwa moto ambao uliwachoma watu.

hawakuliweka moyoni

Kuzingatia kwa makini kwa jambo na kujifunza kwake inazungumziwa kana kwamba walikuwa wakiweka jambo hilo juu ya moyo wa mtu. "hawakuzingatia kwa makini" au "hawakujifunza kutoka kwake"

Isaiah 43

Isaiah 43:1

yeye aliyekuumba wewe, Yakobo, na yeye aliyekutengeneza wewe, Israeli

Vishazi hivi vyote viwili vina maana moja. "yule ambaye amekuumba, Ee watu wa Israeli"

Isaiah 43:2

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Utakapopita katikati ya maji ... miale haitakuangamiza

Yahwe anazungumza kuteseka na kupitia ugumu kana kwamba ni maji marefu na moto ambayo watu hutembea. Maneno "maji" na "miale" huunda neno lenye maana ya mambo mengi na husisitza hali yoyote ngumu.

Utakapopita katikati ya maji, nitakuwa pamoja nawe; na katikati ya maji, hayatakushinda

Kauli hizi mbili zina maana moja na husisitiza y kwamba watu hawatapitia madhara kwa sababu Yahwe yupo pamoja nao.

hautachomwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "haitakuchoma"

Nimewapatia Msri kama fidia yako, Kushi na Seba kubadilishana kwa ajili yako

Misemo hii miwili inatumia maana moja na inasisitiza ya kwamba Yahwe ataruhusu adui wa Israeli kushinda mataifa haya badala ya Israeli.

Seba

Hili ni jina la taifa.

Isaiah 43:4

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Kwa maana una thamani na wa kipekee machoni mwangu

Maneno "thamani" na "kipekee" yana maana moja na yanasisitiza jinsi gani Yahwe huthamini watu wake. "Kwa sababu wewe ni wa thamani kwangu"

kwa hiyo nitawapa watu kwa kubadilishana kwa ajili yako, na watu wengine kwa kubadilishana kwa maisha yako

Misemo yote ina maana moja. "kwa hiyo nitaruhusu adui kuwashinda watu wengine badala yako"

Nitaleta watoto wako kutoka mashariki, kukukusanya kutoka magharibi

Pande "mashariki" na "magharibi" huunda neno lenye maana ya kundi na linawakilisha kila upande. "Nitakuleta wewe na wtoto wako kutoka kila upande"

Isaiah 43:6

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

nitasema kwa kaskazini ... kwa kusini

Yahwe anazungumza kwa "kaskazini" na "kwa kusini" kana kwamba anaamuru mataifa katka maeneo hayo.

wana wangu ... binti zangu

Yahwe anazungumzia wtu ambao wanakuwa wake kana kwamba walikuwa watoto wake.

kila mtu ambaye ameitwa kwa jina langu

Hapa kuitwa kwa jina la mtu inawakilisha kuwa mali ya mtu huyo. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "kila mtu ambaye nimemuita kwa jina langu" au "kila mtu ambaye ni mali yangu"

ambaye nimemuumba, ndio, ambaye nimemtengeneza

Zote hizi zina maana moja na husisitiza ya kwamba ni Mungu ambaye aliwatengeneza watu wa Israeli.

Isaiah 43:8

watu ambao ni vipofu ... viziwi

Yahwe anazungumzia wale ambao hawamsikilizi au kumtii kana kwamba walikuwa vipofu na viziwi.

Ni nani kati yao angeweza kutamka hili na kutangaza kwetu matukio ya mapema?

Swali hili la balagha linatumika kwa miungu ambao watu wa mataifa huabudu. Jibu linalodokezwa ni kwamba hakuna kati yao angefanya hivi. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Hakuna kati ya miungu yao ingeweza kutamka hili au kutangaza kwetu matukio ya mapema"

kutangaza kwetu matukio ya mapema

Msemo huu una maana ya uwezo wao kusema juu ya matukio ambayo yametokea kipindi cha nyuma kabla hayatokea. "alitangaza kwetu matukio ya mapema kabla hayajatokea"

Waache walete mashahidi wao kujithibitishia wenyewe kuwa sahihi, waache wasikilize na kukiri, "Ni ukweli'.

Yahwe anatoa changamoto kwa miungu ambao mataifa huabudu kutoa mashahidi ambao watashuhudia ya kwamba wameweza kufanya vitu hivi, ingawa anajua ya kwamba hawawezi kufanya hivyo. "Miungu hawa hawana mashahidi ambao watathibitisha kuwa sahihi, mashahidi ambao watasikiliza na kukiri, "Ni kweli"

Isaiah 43:10

Nyie ... mtumishi wangu

Hapa "nyie" ni wingi na ina maana ya watu wa Israeli. Msemo "mtumishi wangu" ina maana ya taifa, kwa ukamilifu.

Kabla yangu ... baada yangu

Kwa kuzungumza kwa njia hii, Yahwe hasemi ya kwamba kulikuwa na muda ambapo hakuwepo au kipindi ambacho hatakuwepo. Anasema ya kwamba yeye ni wa milele na kwamba miungu ambayo watu wa mataifa mengine huabudu hawako hivyo.

Kabla yangu hapakuwa na miungu aliyeumbwa

Hapa neno "kumba" inaonyesha ya kwamba Yahwe anazungumzia sanamu ambazo watu waliumba. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Hakuna kati ya miungu ambao watu walitengeneza walikuwepo kabla yangu"

na hapatakuwa naye baada yangu

"na hakuna kati ya miungu hao atakuwepo baada yangu"

Mimi, mimi ni Yahwe

Neno "Mimi" inarudiwa kusisitiza lengo kwa Yahwe. "Mimi pekee ni Yahwe" au "Mimi mwenyewe ni Yahwe"

hakun mkombozi ila mimi

Hii inaweza kuelezwa kwa chanya. "Mimi ni mkombozi pekee" au "Mimi ndiye pekee mbaye naweza kukuokoa"

Isaiah 43:12

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

hakuna atakayeweza kuokoa yeyote kutoka mkononi mwangu

Hapa neno "mkono" linawakilisha nguvu ya Yahwe. "hakuna mtu anaweza kuokoa yeyote kutoka kwa nguvu yangu"

nani anawvza kugeuza?

Yahwe anatumia swali hili kusema ya kwamba hakuna mtu anaweza kugeuza mkono wake. Inaweza kutafsiriwa kam kauli. Kugeuza mkono wake inawakilisha kumzuia kutofanya kitu. "hakuna ambaye ataigeuza" au "hakuna mtu anaweza kunizuia"

Isaiah 43:14

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Mtakatifu wa Israeli

Mtakatifu wa Israeli

Nimetuma Babeli na kuwaongoza wote chini

Kitu cha kitenzi "tuma" kinaweza kutumika katika tafsiri. "Ninatuma jeshi Babeli"

kuwaongoza wote chinii kama wakimbizi

"ongoza Wababeli wote chini kama wakimbizi"

wakimbizi

Mkimbizi ni mtu ambaye hukimbia mbali ili adui yake asiweze kumkamata.

Isaiah 43:16

ambaye alifungua njia ... kama utambi unaowaka

Katika mistari hii, Isaya anazungumzia matukio yanayofuata safari kutoka Misri, Yahwe alipogawanya bahari kuruhusu Waisraeli kutembea katikati juu ya nchi kavu lakini kisha kuzamisiha jeshi la Wamisri. Maana kamili ya kauli inaweza kuwekwa wazi.

Walianguka chini pamoja; hawatainuka tena

Kufa inazungumziwa kana kwamba ilikuwa kuanguka chini ardhini. "Wote walikufa pamoja; hawataishi tena"

wamezimwa, wamepozwa kama utambi unaowaka

Watu kufa inazungumziwa kana kwamba walikuwa wakichoma mshumaa wa utambi ambayo mtu ameuzima. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "maisha yao yamekwisha, kama mtu anavyozima mwale wa mshumaa unaowaka"

Isaiah 43:18

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Usiwaze juu ya vitu hivi vya awali, wala kufikiria vitu vya zamani sana

Misemo hii miwili ina maana moja na kusisitiza ya kwamba hawapaswi kuwa na wasiwasii juu ya kilichotokea kipindi cha nyuma.

Tazama

Hii ni lahaja. "Sikiliza" au "Zingatia kwa makini"

je! hauielewi?

Yahwe anatumia swali kufundisha watu wa Israeli. Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "hakika umeigundua"

Isaiah 43:20

wanyama pori wa mashamba wataniinua mimi, mbweha na mbuni

Hapa wanyama wanamheshimu Yahwe kana kwamba walikuwa watu.

mbweha na mbuni

Hawa ni mifano ya aina ya wanyama ambao watamheshimu Yahwe. "mbweha na mbuni wataniheshimu"

Isaiah 43:22

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Isaiah 43:24

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

ufito wa mwanzi wenye manukato

ufito wa mwanzi wenye manukato Huu ni mmea wenye harufu nzuri inayotumika kutengeneza mafuta ya kupaka. Haikuota katika nchii ya Israeli kwa hiyo watu walitakiwa kuinunua kutoka mataifa mengine.

umenibebesha mzigo na dhambi zako, umenichosha na matendo yako maovu

Zote hizi zina maana moja na husisitiza malalamiko ambayo Yahwe anayo kwa watu wake.

umenibebesha mzigo na dhambi zako

"umenihangaisha na dhambi zako"

Isaiah 43:25

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Mimi, ndio, mimi

Neno "Mimi" linarudiwa kwa ajili ya msisitizo. "Mimi pekee"

anayefuta makosa yako

Kusamehe dhambi inazungumziwa kama kuwa aidha 1) kuziondoa au kuzipangusa mbali au 2) kufuta kumbukumbu iliyoandkwa ya dhambi. "ambaye husamehe makosa yako kama mtu anayepangusa kitu mbali" au "ambaye husamehe makosa yako kama mtu ambaye hufuta kumbukumbu ya dhambi"

kwa ajili yako

"kwa ajili ya heshima yangu" au "kwa ajili ya sifa yangu"

sitaweka akilini

"kumbuka"

wasilisha kesi yako, ili uweze kuthibitishwa hauna hatia

Yahwe anawapa changamoto watu kutoa ushahidi ya kwamba hawana hatia kwa mashtaka ambayo ameleta dhidi yao, ingawa anajua hawawezi kufanya hivyo. "wasilish kesi yako, lakini huwezi kuthibitisha kuwa hauna hatia"

ili uweze kuthibitishwa hauna hatia

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "ili uweze kuthibitisha mwenyewe kuwa huna hatia"

Isaiah 43:27

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Baba yako wa kwanza alitenda dhambi

Hii ina maana ya mwanzilish wa Israeli na inaweza kuwakilisha aidha Abrahamu au Yakobo.

Nitamweka Yakobo katika uharibifu kamili

Hapa "nitamweka" inawakilisha kumweka mtu chini ya nguvu ya mwingine. Nomino ya "uharibifu" inaweza kutafsiriwa kwa msemo wa kitenzi. "Nitasababisha adui kumuangamzia Yakobo kabisa"

Israeli katiika aibu ya shutumu

Kitenzi kinaweza kutumika kutoka msemo wa nyuma, ambayo msemo huu ni sambamba. Nomino "aibu" inaweza kutafsiriwa na msemo wa kitenzi. "Nitaruhusu adui kutukana na kudhalilisha Israeli"

Isaiah 44

Isaiah 44:1

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Yakobo mtumwa wangu

Hii ina maana ya uzao wa Yakobo. "vizazi vya Yakobo, watumishi wangu"

yeye aliyekutengeneza na kukuumba ndani ya tumbo

Yahwe anazungumzia kuumba taifa la Israeli kana kwamba alikuwa akiumba taifa kama mtoto katika tumbo lake. "yeye aliyekutengeneza, kama navyoumba mtoto ndani ya tumbo"

na wewe, Yeshuruni, ambaye nimekuchagua

Kitenzii kinaweza kutumika kutoka kwa msemo uliopita. "na wewe, Yeshuruni, ambaye nimekuchagua, usiogope"

Yeshuruni

Hii pia ina maana ya watu wa Israeli.

Isaiah 44:3

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Nitamwaga maji katika ardhi yenye kiu, na vijito vinavyotiririka juu ya ardhi kavu

Yahwe anazungumza kutoa Roho wake kwa wtu wa Israeli kana kwamba alikuwa akisababisha mvua kuanguka na vjito kutiririka juu ya ardhi kavu.

ardhi yenye kiu

Ardhi kavu inazungumziwa kana kwamba ilikuwa mtu mwenye wivu. "ardhi kavu"

nitamwaga Roho wangu juu ya watoto wako

Yahwe anazungumza kumtoa Roho wake kwa watu kana kwmba Roho wake alikuwa kimiminiko ambacho alimwaga juu yao. "Nitatoa Roho wangu kwa watoto wao"

na baraka yangu juu ya wtoto wako

Kitenzi kinaweza kutolewa kutoka katika msemo wa nyuma. "na nitamwaga baraka yangu juu ya watoto wako" au "na nitatoa baraka yangu kwa watoto wangu"

Watachipuka juu katika nyasi, kama mierebi kando na vijito vya maji

Watu wa Israeli kuwa na mafanikio na kuongezeka inazungumziwa kana kwamba walikuwa mimea ambayo huota kwa sababu wana majii mengi.

mierebi

Muerebi ni mti wenye matawi membamba ambayo huota kaaribu na maji.

Isaiah 44:5

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

mwingine ataita jina la Yakobo

"mtu mwingine atasema kuwa yeye ni uzao wa Yakobo"

kujiita mwenyewe kwa jina la Israeli

"kujita mwenyewe uzao wa Israeli"

Isaiah 44:6

Mkombozi wake

"Mkombozi wa Israeli"

Yahwe of majeshi

Yahwe of majeshi wa Israeli

Mimi ni wa kwanza, na mimi ni wa mwisho

Msemo huu unasisitiza asili ya Yahwe ya milele. Maana zaweza kuwa 1) "Mimi ndiye ambaye nilianzisha vitu vyote, na mimi ndiye ambaye humaliza vitu vyote" au 2) "Mimi ndiye yule ambaye niliishi daima, na mimi ndiye yule ambaye nitaishi daima"

Isaiah 44:7

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza

Nani kama mimi? Na atangaze

Yahwe anatumia swali hili la balagha kusisitiza ya kwamba hakuna mtu kama yeye. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli. "kama yeyote anafikiri ni kama mimi, na atangaze"

Isaiah 44:8

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Usiwe na hofu au kuogopa

Yahwe anatumia misemo miwili ya kufanana ili kuimarisha faraja yake. "Usiogope"

Je! sijatamka kwako zamani, na kuitangaza?

Yahwe anatumia swali hili kusisitiza ya kwamba yeye ndiye ambaye alitabiri matukio ambayo yametokea sasa. Hii inaweza kutafsiriwa kama kauli. Neno "kutangaza" lina maana ya kitu kimoja kama "kutangaza". "Nimetangaza mambo haya kwako zamani"

Je! kuna Mungu yeyote kando ya mimi?

Yahwe anatumia swali tena kusisitiza ya kwamba hakuna Mungu mwingine. Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Hakuna Mungu kando ya mimi"

Hakuna Mwamba mwingine

Yahwe anajizungumzia kana kwamba alikuwa jiwe kubwa ambayo chini yake wtu wanaweza kupata hifadhi. Hii ina maana ya nguvu kulinda watu wake.

Isaiah 44:9

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza

vitu wanavyofurahia navyo havina thamani

"sanamu wanazozifurahia hazina thamani"

mashahidi wao hawawezii kuona au kujua chochote

Msemo huu una maana ya wale ambao huabudu sanamu hawa na kudai kuwa mashahidi wa nguvu ya sanamu. Yahwe anazungumzia ukosefu wa uwezo wao kuelewa ukweli kana kwamba walikuwa vipofu. "wale ambao hutumika kama mashahidi kwa ajili ya sanamu hizi ni kama watu vipofu ambao hawajui chochote"

wataaibishwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "wataaibika" au "sanamu zao zitaaibishwa"

Nan angeweza kuunda mungu au kuchonga sanamu ambayo haina thamani?

Yahwe anatumia swali hili kukemea wale ambao hutengeneza sanamu. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Ni wapumbavu pekee wanaweza kuunda mungu au kuchonga sanamu ambayo haina thamani"

kuchonga sanamu ambayo haina thamani

Neno "haina thamani" haitofautishi kutofaa kwa sanamu kwa sanamu ambazo zina thamani, kwa sababu sanamu zote hazina thamani. "kuchonga sanamu ambazo hazina thamani"

Isaiah 44:11

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza

washiriki wake wote

Maana zaweza kuwa 1) hii ina maana kuwa washiriki wa fundistadii ambaye hutengeneza sanamu. "washiriki wote wa fundistadi" au 2) hii ina maana ya wale washiriki wenyewe pamoja na sanamu kwa kuiabudu. "wale wote ambao huabudu sanamu"

wataaibishwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "ataaibika"

Acha wachukue msimamo wo pamoja

"Waache wote waje pamoja mbele zangu"

wataogopa

"watogopa". "kuogopa" ni kuinama mbele kwa hofu.

Isaiah 44:12

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza

kuiunda

"kuunda sanamu" au "kutengeneza sanamu"

Isaiah 44:13

kwa kamba

Kamba iliyotumika kuchora mstari umbo la sanamu katika mbao.

sindano ya santuri

Hiki ni chombo chenye ncha kali kukwaruza mbao ili fundistadi aweze kuona wapi pa kukata.

bikari

Hiki ni chombo chenye ncha sehemu mbili ambacho hutandazwa kusaidia kuweka alama katika mbao kutengeneza sanamu.

Isaiah 44:14

Hukata chini

"Fundi seremala hukata chini" au "mchonga mbao hukata chini"

mvinje

mti mrefu wa majani ya kijani

Isaiah 44:15

Kisha mtu huitumia

"Mwanamume hutumia mbao"

hutengeneza sanamu na kuinama chini kwake

Sehemu hii ya sentensi kimsingi inasema jambo moja kama ya kwanza kusisitiza.

Isaiah 44:18

kwa maana macho yao ni vipofu na hayawezi kuona

Yahwe anazungumzia watu ambao hawawezi kuelewa upumbavu wa kuabudu sanamu kana kwamba walikuwa vipofu.

kwa maana macho yao ni vipofu

Hapa "macho yao" yanawakiilisha mtu mzima. "kwa maana ni vipofu"

mioyo yao haiwezi kutambua

Hapa neno "mioyo" inawakilisha akili na mawazo ya watu. "hawawezi kuelewa"

Isaiah 44:19

Sasa naweza kutengeneza ... kitu cha kuchukiza cha kuabudu? Je! nitainama chini kwa kipande cha mbao?

Yahwe anasema ya kwamba watu hawa wanatakiwa kujiuliza maswali haya ya balagha. Maswali yanatazamia majibu ya kukana na kusisitiza jinsi itakavyokuwa upumbavu kwa mtu kufanya mambo haya. Maswali haya yanaweza kutafsiriwa kama kauli. "Sitakiwi sasa kutengeneza ... kitu cha kuchukiza cha kuabudu. Sitakiwi kuinama chini kwa kipande cha mbao"

Isaiah 44:20

Ni kana kwamba alikuwa akila majivu

Yahwe anazungumzia mtu kuabudu sanamu kana kwamba mtu huyo alikuwa akila majivu yaliiyochomwa ya mbao kutoka pale alipotengenezea sanamu. Kama vile kula majivu haimpi mtu faida, wala kuabudu sanamu.

moyo wake uliodanganywa humpotosha

Moyo unawakilisha undani wa mtu. "anajipotosha kwa sababu amedanganywa"

Hawezi kujiokoa mwenyewe

"Mtu ambaye huabudu sanamu hawezi kujiokoa mwenyewe"

Isaiah 44:21

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza

Yakobo, na Israeli

Hii ina maana ya watu waliotokana kwa Yakobo, Israeli. "nyie uzao wa Israeli"

hautasahaulika na mimi

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Sitakusahau"

Nimefuta, kama wingu zito, matendo yako ya uasi, na kama wingu, dhambi zako

Kauli hizi mbili zina maana ya kitu kimoja. Mungu ameondoa dhambi zao kwa haraka na urahisi kama upepo uweze kupuliza mbali wingu.

na kama wingu, dhambi zako

Kitenzi kinaweza kutumika kutoka na msemo uliopita. "na kama wingu, nimefuta dhambi zako"

Isaiah 44:23

Imbeni, enyi mbingu ... utukufu wake katika Israeli

Hapa Isaya anazungumzia sehemu mbalimbali za uumbaji kana kwamba walikuwa watu na kuwaamuru kumsifu Yahwe.

enyi vina virefu vya dunia

"enyi sehemu za chini za dunia". Maana zaweza kwa 1) ya kwamba hii ina maana ya sehemu zenye vina virefu sana katika dunia kama vile mapango au makorongo na kuunda neno linalowakilisha kundi la maneno kama "mbingu" katika msemo uliopita au 2) ya kwamba hii ina maana ya sehemu ya wafu.

Isaiah 44:24

Mkombozi

Mkombozi wa Israeli

yeye aliyekuumba katika tumbo

Yahwe anazungumzia kuumba taifa la Israeli kana kwamba ilikuwa kuunda taifa kama mtoto katika tumbo la mama yake. "yeye aliyekuumba, kama navyouumba mtoto katika tumbo"

ambaye yeye peke yake alitandaza mbingu

Yahwe anazungumzia kuumba mbingu kana kwamba ilikuwa nguo ambayo ilitandazwa.

ishara

Hizi ni ishara ambazo watu walitumia kujaribu kutabiri siku za usoni.

waongea watupu

Hii ina maana ya watu ambao husema vitu ambavyo havina maana.

Isaiah 44:26

nani alithibitisha maneno ya mtumishi wake na kuyafanya kutendeka utabiri wa wajumbe wake

Yahwe anasema jambo moja mara mbili kusisitiza ya kwamba ni yeye pekee, Yahwe, ambaye husababisha unabii kutimia.

maneno ya mtumishi wake ... utabiri wa wajumbe wao

Nomino dhahania "maneno" na "utabiri" inaweza kutafsiriwa kama vitenzi. "kile mtumishi wake atakavyotamka ... kile wajumbe wake wanachotangaza"

Atafanyiwa makazi

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Watu wataishi pale tena"

Itajengwa tena

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Watu wataijenga tena"

Nitainua uharibifu wao

Msemo "uharibifua" ina maana ya sehemu ambazo zimeangamizwa. Yahwe anazungumza kuijenga tena kana kwamba alikuwa akiinua. "Nitajenga tena kile wengine walichoangamiza"

Isaiah 44:28

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza

Yeye ni mchungaji wangu

Yahwe anazungumzia Koreshi kutawala na kulinda watu wa Israeli kana kwamba Koreshi ni mchungaji wao.

Acha ijengwe tena

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. 'Acha watu wajenge tena mji"

Acha msingi wako ulazwe

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Acha watu walaze misingi yake"

Isaiah 45

Isaiah 45:1

ambao mkono wake naushikilia

Yahwe kuwasaidia Koreshi na kumsababishia kufanikiwa inazungumziwa kana kwamba alikuwa akishikilia mkono wake wa kuume.

Isaiah 45:2

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na Kosheri.

na kusawazisha milima

Yahwe anazungumza kuondoa vizuizi ambavyo vinaweza kukawiza mafanikio ya Koreshi kana kwamba ilikuwa kusawazisha milima mbele yake.

milima

Neno la Kiebrania linalotumika katika maandishi ni adimu na maana haileweki. Baadhi ya tafsiri zina "sehemu za kukwaruzakwaruza" au "sehemu zilizopinda".

nguzo zao za chuma

Hii ina maana ya nguzo za chuma katika malango ya shaba.

hazina za giza

Hapa "giza" ina maana ya sehemu ambazo ni za siri. "hazina katika sehemu za giza" au "hazina katika sehemu za siri"

Isaiah 45:4

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na Koreshi.

Yakobo ... Israeli

Zote hizi zina maana ya vizazi vya Israeli.

Nitakuandaa kwa ajili ya vita

Maana zaweza kuwa 1) "Nitakuimarisha kwa ajili ya vita" au 2) "Nitakuandaa kwa ajili ya vita"

kutoka katika kuchomoza kwa jua, na kutoka magharibi

Kwa kuwa jua huzama mashariki, msemo huu unaunda neno kwa ajili ya maneno mengine na ina maana ya kila sehemu juu ya dunia. "kutoka kila sehemu duniani"

Isaiah 45:7

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza.

Ninaunda nuru na kuumba giza; Ninaleta amani na kuumba maafa

Misemo hii miwili inaunda neno kwa ajili ya maneno mengine ambayo inasisitiza ya kwamba Yahwe ni muumba wa enzi wa kila kitu.

Enyi mbingu, nyesha chini kutoka juu ... haki huruka juu pamoja nayo

Yahwe anazungumzia haki yake kana kwamba ilikuwa mvua ambayo huanguka juu ya ardhi, na ya haki yake na wokovu kama mimea ambayo huota juu ya dunia.

Enyi mbingu

Yahwe kwa muda anageuza akili yake kutoka kwa watu wake na kuanza kuzungumza kwa mbingu.

Isaiah 45:9

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza

chungu kingine cha duniani kati ya vyungu vya duniani katika ardhi

Yahwe anazungumza juu yake kana kwamba alikuwa mfinyanzi, na kwa yule ambaye angebishana naye kana kwamba mtu huyo na binadamu waliosalia waliikuwa vyungu vya udongo. "kama kipande kimoja cha ufinyanzi katika vipande vingi vingine vya ufinyanzi vilivyosambaa juu ya ardhi"

chungu cha dunia

Maana zaweza kuwa 1) "chungu cha udongo" au 2) "kipande kilichovunjika cha ufinyanzi wa udongo".

Je! udongo husem kwa mfinyanzi ... juu yake'?

Yahwe anauliza swali hili kukarpia wle ambao hubishana naye juu ya kile anachofanya. "Udongo haupaswi kusema kwa mfinyanzi ... juu yake!"

Isaiah 45:10

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kukaripia wale ambao hubishana na yeye kuhusu kile anachofanya.

Ole wake asemaye kwa baba, ... 'Unazaa kitu gani?'

Yahwe anazungumzia wale ambao wangebishana naye kana kwamba walikuwa watoto ambao hawajazaliwa ambao hubishana na wazazi wao wenyewe.

Unalea kitu gani? .... Unazaa kitu gani?

Mtoto ambaye hajazaliiwa anauliza maswali haya ya balagha kukaripia wazazi wake kwa kumzaa. Hii naweza kutafsiriwa kama kauli. "Hautakiwi kuwa baba yangu ... Hautakiwi kunizaa mimi" au "Haunileii kwa usahihi ... Haunizai kwa usahihi".

Isaiah 45:11

Mtakatifu wa Israeli

Mtakatifu wa Israeli

Kwa nini unauliza maswali kuhusu kile nitakachofanya kwa ajili ya watoto wangu? Je! utaniambia nini cha kufanya kuhusu kazi ya mikono yangu?

Yahwe anatumia maswali kukaripia wale ambao wanabishana naye kuhusu kile anachofanya. "Usiniulize mimi kuhusu kile ninachofanya kwa ajili ya watoto wangu. Usiniambie ... mikono yangu".

watoto wangu

Hii ina maana ya watu wa Israeli.

kazi ya mikono yangu

Hapa neno "mikono" linawakilisha Yahwe. "vitu ambavyo nimevitengeneza"

Isaiah 45:12

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza.

Ilikuwa mkononi mwangu ya kwamba

Hapa neno "mikono" inawakilisha Yahwe. "Ilikuwa mimi ambaye"

iliyotandaza mbingu

Yahwe anazungumza kuumba mbingu kana kwamba zilikuwa kitambaa ambacho alikitandaza nje.

Isaiah 45:13

Taarfa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza.

Nilimwamsha Koreshi wima katika haki

Hapa neno "haki" lina maana ya matendo sahihi. Maana zaweza kuwa 1) ambayo Yahwe amemwamsha Koreshi kufanya jambo sahihi au 2) ambalo Yahwe alikuwa sahihi kumwasha Koreshi

Nilimwamsha Koresh

Yahwe anazungumzia kusababisha Koreshi kutenda kana kwamba alikuwa akiamshwa kutoka usiingizini

Nitalaiinsha njia zake zote

Yahwe anazungumzia kuondoa vikwazo na kusababisha Koreshi kuwa na mafanikio kana kwamba alikuwa akitengeneza njia laini ambazo Koreshi anatembelea.

Atajenga mji wangu

Hii ina maana ya Yerusalemu.

na sio kwa gharama wala rushwa

Hapa maneno "gharama" na "rushwa" hutumia maana moja. Koreshi hatafanya vitu hivi kwa ajili ya faida ya mapato. "na hatafanya vitu hivi kwa ajili ya fedha"

Yahwe wa majeshi

Yahwe wa majeshi ya Israeli

Isaiah 45:14

Mapato ya Misri na bidhaa za Ethiopia pamoja na Waseba, wanaume wa maumbile marefu, wataletwa kwako

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "'Watu wa Misri, Ethiopia, na watu warefu wa Seba, watakuletea mapato yako na bidhaa zao"

Mapato ya Misri

"Faida za Misri"

Waseba

Watu hawa kutoka taifa la Seba.

kwako

Hapa "kwako" ina maana ya watu wa Yerusalemu.

Isaiah 45:16

Wataaibika na kufeheshwa pamoja; wale wanaochonga sanamu watatembea kwa aibu

Mistari hii miwili inatumia maana moja, na wa pili kufafanua neno la mstari wa kwanza

Wataaibika na kufeheshwa pamoja

Maneno "aibishwa" na "fedheheshwa" kwa msingi yana maana moja na husisitiza ukali wa aibu. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Sanamu zao zitawaacha wote na aibu kabisa"

watatembea kwa aibu

Kuishi katika aibu ya muendelezo inazungumziwa kana kwamba ilkuwa kutembea katika aibu. "ataendelea kuabishwa"

Israeli ataokolewa na Yahwe

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. 'Yahwe atawaokoa watu wa Israeli"

hautakuwa tena na aibu au fedheha

Hapa "hautakuwa" ina maana ya watu wa Israeli. Maneno "aibu" na "fedheha" ina maana ya kitu kimoja. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Hakuna mtu atakayekuaibisha tena"

Isaiah 45:18

sio kama takataka

"ili isiwe tupu". Hapa neno "takataka" lina maana ya sehemu tupu, isiyozaa.

lakini aliiunda ili ikaliwe

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "lakini aliiunda ili watu waweze kuishi juu yake"

Isaiah 45:19

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza.

Isaiah 45:20

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza

wakimbizi

watu ambao wametoroka kutoka katika nyumba zao ili adui wasiwakamate au kuwaua

Isaiah 45:21

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza kwa wakimbizi.

Na waache waungane pamoja

Hapa neno "waache" na maana ya wakimbizi kutok miongoni mwa mataifa ambao huabudu sanamu.

Ni nani ameonyesha hili kutoka zamani? Nani amelitangaza? Je! haikuwa mimi, Yahwe?

Yahwe anatumia maswali kusisitiza ya kwamba yeye ndiye aliyewaambia vitu hivi vingetokea. "'Nitawaambia ni nani aliyewaonyesha haya tangu zamani. Nitawaambia ni nani aliyeitangaza. Ilikuwa ni mimi, Yahwe"

Isaiah 45:22

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza.

Geukia kwangu na ukolewe

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "'Geuka kwangu nami nitakuokoa"

mwisho wote wa dunia

Sehemu za dunia ambazo zipo mbali sana zinazungumziwa kana kwamba zilikuwa sehemu ambapo dunia hufika mwisho. Msemo huu pia hunda neno kwa ajili ya maneno mengine kwa ajili ya kila seheu katikati ya mwisho. "sehemu zote za mbali za dunia" au "dunia nzima"

mwisho wote wa dunia

Hapa msemo huu unawakilisha watu ambao wanaishi katika "mwisho wa dunia". "nyie ambao mnaishi katika sehemu za mbali za dunia" au "'nyie wote mnaoishi juu ya dunia"

Kwangu kila goti litainama, kila ulimi utaapa

Maneno "goti" na "ulimi" yanawakilisha watu. "Kila mtu atapiga goti mbele yangu, na kila mtu ataapa"

Isaiah 45:24

Wanasema

Watu wote wa dunia wanazungumza

Katika Yahwe vizazi vyote wa Israeli watafanywa kuwa haki

Hapa neno "kufanywa kuwa haki" haimaanisha Yahwe kusamehe dhambi zao, lakini kuthibitisha kwa mataifa ambayo Israeli alikuwa sahihi kumwabudu yeye. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe atavifanya kuwa haki vizazi vyote vya Israeli" au "Yahwe atathibitisha vizazi vyote vya Israeli"

Isaiah 46

Isaiah 46:1

Beli anainama chini, Nebo anajishusha; sana zao ... kwa wanyama waliochoka kuishi

Isaya anazungumzia watu kuweka sanamu ya Beli na Nebo katika mkokoteni wa wanyama kusafirisha kana kwamba bidhaa hizi zilifanywa "kuinama chini" na "kujishusha". Hii yote ni mikao miwili ya kufedhehesha.

Beli ... Nebo

Hawa walikuwa miungu miwili wa msingi ambao Wababeli waliwaabudu.

sanamu zao

sanamu ambazo ziliakilisha Beli na Nebo

hawawezi kuokoa sanamu

"Beli na Nebo hawawezi kuokoa sanamu zao"

wao wenyewe wamekwenda katika kifungo

Isaya anazungumzia watu kubeba sanamu hizi kana kwamba miungu ya uongo ambayo inawakilisha inabebwa katika kifungo.

Isaiah 46:3

Nisikilize mimi

Hapa "mimi" ina maana ya Yahwe

ambao wamebebwa na mimi kabla ya kuzaliwa kwako, kubebwa kutoka tumboni

Yahwe anazungumzia taifa la Israeli kana kwamba lilikuwa mtu, na mwanzo wa taifa kana kwamba ni kuzaliwa kwake.

ambao wamebebwa na mimi

Yahwe anazungumzia kusaidi na kuokoa watu wa Israeli kana kwamba alikuwa akiwabeba. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ambao nimewabeba"

Hata katika uzee wako mimi ndiye, na mpaka nywele zako ni mvi nitakubeba

Yahwe anazungumzia taifa la Israeli kuwa zee sana kana kwamba likikuwa mwanamume mzee mwenye mvi.

Isaiah 46:5

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Utanilinganisha na nani? Ni nani unadhani nafanana naye, ili kwamba tuweze kulinganishwa?

Yahwe anatumia swali kusisitiza ya kwamba hakuna mtu kama yeye. "hakuna mtu ambaye mnaweza kunilinganisha naye. Sifanani na mtu, ili tuweze kulinganishwa"

ili kwamba tuweze kulinganishwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ili uweze kutulinganisha"

Isaiah 46:7

Wanaiinua

"Wana..." ina maana ya watu ambao hutengeneza sanamu na "..iinua" ina maana ya sanamu ambayo wametengeneza.

Isaiah 46:8

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wake.

Isaiah 46:10

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wake.

Ninatangaza mwisho kutoka mwanzo, na kabla ya muda kile ambacho hakijatokea

Hii kwa msingi inarudia wazo hilo hilo kwa msisitizo. Kitenzi kutoka katika msemo wa kwanza unaweza kutumika kwa msemo wa pili. "Ninatangaza mwisho kutoka mwanzo, na ninatangaza kabla ya muda kile ambacho bado hakijatokea"

Ninamwita ndege wa mawindo kutoka mashariki

Yahwe anazungumzia Kipro kana kwamba ilikuwa "ndege wa mawindo". Kama ndege anavyokamata kwa haraka windo lake, kwa hiyo Kipro itatimiza kusudi la yahwe kushinda mataifa.

Nimesema; Nitaitimiza pia; Nimekusudia, nitaifanya pia.

Hii inarudia wazo hilo hilo kwa ajili ya msisitizo.

Isaiah 46:12

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

ambao wako mbali na kufanya kilicho sahihi

Yahwe anazungumzia watu kufanya mabaya kwa ukaidi kana kwamba walikuwa mbali kihalisia na kufanya kilicho chema.

wokovu wangu hausubiri

Yahwe anazungumzia kuokoa watu wake mapema kana kwamba wokovu wake ulikuwa mtu ambaye hasubiri kutenda. "Sitasubiri kukuokoa"

Isaiah 47

Isaiah 47:1

Taarifa ya Jumla

Katika sura hii, Yahwe anazungumza na Babeli kuhusu anguko lake kana kwamba alikuwa malkia ambaye ameaibishwa.

keti katika vumbi, binti bikira wa Babeli; keti juu ya ardhi ... binti wa Wakaldayo.

Misemo hii miwili ina maana moja. Kuketi katika mavumbi ni ishara ya aibu.

binti bikirawa Babeli ... binti wa Wakaldayo

Misemo hii miwili ina maana ya mji, Babeli, ambao unazungumziwa kana kwamba ilikuwa binti. Ya kwamba mji ni "binti" ikionyesha jinsi watu wanavyofikiri kwa kubembeleza juuyake.

bila kiti cha enzi

Hapa "kiti cha enzi" ina maana ya nguvu ya kutawala. "bila nguvu ya kutawala"

Hautaitwa tena mrembo na wa kuvutia

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Watu hawatakuita tena mrembo na wa kuvutia"

mrembo na mzuri

Maneno haya mawili yanatumia maana moja. Wanafafanua yule ambaye ni mzuri na anaishi katika starehe. "mzuri sana" au "mwenye starehe sana"

jiwe la kusaga

jiwe kubwa linatumiwa kusaga nafaka

Isaiah 47:3

Kauli Kiunganishi

Yahwe anaendelea kuzungumza na Babeli kuhusu anguko lake kana kwamba alikuwa malkia ambaye ameaibishwa.

Uchi wako utafunuliwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Utakuwa uchi"

aibu yako itaonekana

Hapa neno "aibu" ni tasifida kwa ajili ya sehemu za siri za mtu. Hii inaweza kutafsiriwa katika hali ya kutenda. "watu wataona aibu yako" au "watu wataona sehemu zako za siri"

Mkombozi wetu

"wetu" ina maana ya Isaya na watu wa Israeli.

Yahwe wa majeshi

Yahwe wa majeshi ya Israeli

Mtakatifu wa Israeli

Mungu wa Israeli

binti wa Wakaldayo

Msemo huu una maana ya mji, Babeli, ambao unazungumziwa kana kwamba ulikuwa binti. Ya kwamba mji ni "binti" inaashiria jinsi Wakaldayo wanavyomfikiria yeye.

kwa maana hautaitwa tena

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "kwa maana watu hawatakuita tena"

malkia wa falme

Yahwe anazungumzia Babeli kuwa mji mkuu wa Falme ya Babeli kana kwamba ilikuwa malkia aliyetawala falme nyingi.

Isaiah 47:6

Kauli Kiunganishi

Yahwe anaendelea kuzungumza na Babeli kuhusu anguko lake kana kwamba alikuwa malkia ambaye ameaibishwa.

Nilikasirishwa

Hapa "nilikasirishwa" ina maana ya Yahwe.

nilitia unajisi urithi wangu

Yahwe anazungumzia watu wa Israeli kuwa milki yake maalumu kana kwamba walikuwa urithi wake. "Niliwanajisi watu wangu, ambao walikuwa milki yangu maalumu"

kuwakabidhi mikononi mwako

Hapa neno "mkononi" inawakilisha nguvu na utawala wa Babeli. "Ninawaweka chini ya nguvu yako"

umeweka nira nzito sana juu ya watu wazee

Yahwe anazungumzia Wababeli kuwakandamiza watu wazee kana kwamba wamewatendea watu wazee kama ng'ombe na kuweka nira nzito juu ya shingo zao.

nitatawala milele kama malkia wa enzi

Babeli inazungumzia kutawala kwa kudumu juu ya mataifa mengi kana kwamba ilikuwa malkia ambaye atatwala milele.

Hukuviweka vitu hivi moyoni

Yahwe anazungumzia juu ya kufikiria kwa makini kuhusu kitu kana kwamba ilikuwa ni kuweka kitu hicho ndani ya moyo wa mtu. "Haukufikiria vitu hivi"

Isaiah 47:8

Kauli Kiunganishi

Yahwe anaendelea kuzungumza na Babeli kuhusu anguko lake kana kwamba alikuwa malkia ambaye ameaibishwa.

wewe upendaye anasa

"wewe mwenye starehe". Hii ina maana ya starehe nyingi ambazo Babeli alifurahia.

kwa imara

Hii ina maana ya dhana ya usalama ya uongo ya Babeli katika kuwaza ya kwamba hatapoteza nafasi yake ya utajiri na heshima. "unayedhani upo salama"

Sitawahi kukaa kama mjane ... kupotewa kwa watoto

Babeli kuamini ya kwamba mataifa mengine hawataweza kumshinda inazungumziwa kana kwamba hatawahi kuwa mjane au hatawahi kufiwa na watoto.

Sitawahi kukaa kama mjane

"Sitawahi kuwa mjane"

katika muda mmoja katika siku moja

"ghafla katika wakati mmoja"

Isaiah 47:10

Kauli Unganishi

Yahwe anaendelea kuzungumza na Babeli kuhusu anguko lake kana kwamba alikuwa malkia ambaye ameaibishwa.

unasema moyoni mwako

Hapa neno "moyoni" lina maana ya utu wa ndani. "unasema kwako mwenyewe"

Maafa yatakuzidi

Yahwe anazungumzia balaa kana kwamba ilikuwa mtu ambaye anakamata Babeli. "Utapitia maafa"

Uharibifu utaanguka juu yako

Yahwe anazungumzia Babeli kuharibiwa kana kwamba uharibifu ulikuwa kitu ambacho huanguka juu ya mji. "Utapitia uharibifu" au "Wengine watakuangamiza"

Janga litakupiga

Yahwe anazungumzia Babeli kupitia janga kana kwamba janga lilikuwa mtu ambaye anapiga Babeli. "Utapitia janga"

Isaiah 47:12

Kauli Unganishi

Yahwe anaendelea kuzungumza na Babeli kuhusu anguko lake kana kwamba alikuwa malkia ambaye ameaibishwa.

Ng'ang'ania kurusha laana zenu ... huenda utatisha mbali maafa

Yahwe anakejeli Babeli kwa kumwambia kuendelea kufanya uchawi wake kuweka mambo mabaya mbali, lakini anajua ya kuwa haitawasaidia.

Isaiah 47:14

Kauli Unganishi

Yahwe anaendelea kuzungumza na Babeli kuhusu anguko lake kana kwamba alikuwa malkia ambaye ameaibishwa.

watakuwa kama mashina ya mabua. Moto utawaunguza

Yahwe analinganisha waganga na wachawi na mabua ambayo huwaka haraka katika moto. Hii ina maana Yahwe atawaangamiza kwa urahisi kama vile moto unavyochoma mashina ya mabua, na kwa hiyo hawana nguvu ya kuokoa Babeli.

mkono wa mwale wa moto

Hapa neno "mkono" unawakilisha nguvu. "nguvu ya mwale wa moto"

Hakuna mkaa wa kuwapa joto na hakuna moto kwa ajili yao kukaa karibu

Yahwe anasisitiza ya kwamba huu ni moto wa kuharibu kwa kusema kwamba sio moto ambao watu hutumia kujipatia joto.

Isaiah 48

Isaiah 48:1

Sikia haya

"Sikiliza ujumbe wangu". Yahwe anazungumza.

nyumba ya Yakobo

Hapa "nyumba" ina maana ya vizazi vya Yakobo. "vizazi vya Yakobo"

ambao wameitwa kwa jina la Israeli

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "ambao kila mtu huwaita watu wa Israeli"

wametokana na mbegu ya Yuda

Msemo huu unasisitiza ya kwamba ni vizazi vya moja kwa moja, vya kimwili vya Yuda. "ni vizazi vya Yuda"

kumsihi Mungu wa Israeli

"kumwita Mungu wa Israeli"

wanajiita wenyewe

Hii ina maana ya wtu wa Israeli. "mnajiita wenyewe"

mji mtakatifu

Hii ina maana ya Yerusalemu.

Yahwe wa majeshi

Yahwe wa majeshi ya Israeli

Isaiah 48:3

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

walitoka kutoka kwa kinywa changu

"Kinywa" ina maana ya mtu kuzungumza. "nilizungumza mambo haya"

musuli wako wa shingoni hukazika kama chuma, na kipaji chako cha uso kama shaba

Yahwe analinganisha kukazwa kwa misuli ya shingo zao na ugumu wa vipaji vyao vya uso kwa ugumu wa chuma na shaba. Hapa, kuwa na shingo iliyokazwa au kipaji cha uso kigumu ni sitiari ambayo ina maana ya watu kuwa wakaidi. "ni kana kwamba shingo zenu ni chuma na vichwa vyenu ni shaba"

nilitamka mambo haya kwako mapema; kabla havijatokea nilikujulisha

Huku ni kusema kitu hicho hicho mara mbili kwa ajili ya msisitizo.

Isaiah 48:6

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

hautakiri kuwa kile nilichosema ni ukweli?

Yahwe anatumia swali kukaripia watu wa Israeli kwa kutokiri kile wanachopaswa kujua ni ukweli. "wewe ni kaidi na hautakiri kile nilichosema ni kweli"

Isaiah 48:8

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

mambo haya hayakufunuliwa kwa masikio yako mapema

Yahwe anazungumzia kufafanua kitu kana kwamba alikuwa akikunjua. Neno "masikio" yanawakilisha watu ambao wanasikiliza. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Sikuelezea mambo haya kwako kabla"

tangu kuzaliwa

Yahwe anazungumzia mwanzo wa mataifa kana kwamba ulikuwa kuzaliwa kwao.

Isaiah 48:9

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli

Kwa ajili ya jina langu nitasitisha hasira yangu

Hapa neno "jina" lina maana ya sifa ya Yahwe. "Kwa ajili ya sifa yangu nitakawiza hasira yangu"

na kwa ajili ya heshima yangu nitajizuia kukuangamiza

Sehemu hii ya sentensi ina maana moja kama sehemu ya kwanza.

Tazama, nilikutakasa, lakinii sio kama fedha; nimekutakasa katika tanuu la mateso

Yahwe anazungumzia kutumia mateso kusafisha watu wake kana kwamba walikuwa vyuma vya thamani na mateso yalikuwa tanuu ambano anawatakasa.

kwa kuwa ninawezaje kuruhusu jina langu kudharauliwa?

Yahwe anatumia swali kusisitiza kuwa hawezi kuruhusu jina lake mwenyewe kudharauliwa. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "kwa maana sitaruhusu yeyote kudharau jina langu"

Isaiah 48:12

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Yakobo, na Israeli

Zote hizi zina maana ya watu wa Israeli.

Mimi ni wa kwanza, mimi pia ni wa mwisho

Msemo huu unasisitiza asili ya milele ya Yahwe. Maana zaweza kuwa 1) "Mimi ndiye niliyeanzisha vitu vyote, na mimi ndiye humaliza vitu vyote" au 2) "Mimi ndiye niliyekuwa nikiendelea kuishi, na mimi ndiye nitakayekuwa nikiendelea kuishi".

mkono wangu umelaza msingi wa dunia, na mkono wangu wa kuume umezinyosha mbingu

Hapa "mkono" una maana ya Yahwe. "Nililaza msingi wa dunia, na nikatandaza mbingu"

msingi wa dunia

Neno "msingi" kawaida ina maana ya umbo la mawe ambalo hutoa mhimili kwa jengo kutoka chini. Hapa inafafanua umbo ambalo ilidhaniwa kushikilia dunia katika nafasi yake.

umezinyosha mbingu

Yahwe anazungumzia kuumba mbingu kana kwmaba zilikuwa kitambaa ambacho Yahwe alinyosha nje.

ninapoziita, zinasimama juu pamoja

Kusimama pale Yahwe anapoita ni sitiari kwa kuwa tayari kumtii. Yahwe anazungumzia dunia na mbingu kana kwamba ziliweza kumsikia na kumtii.

ninapoziita

Maana zaweza kuwa 1) "ninapoziita dunia na mbingu" au 2) "ninapoziita nyota na mbingu"

Isaiah 48:14

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Nani kati yenu ametanganza mambo haya?

Yahwe anatumia swali kusisitiza ya kwamba sanamu hazijawaambia mambo haya. "Hakuna kat ya sanamu zenu zimesema haya kwenu"

Mshirika wa Yahwe atatimiza kusudi lake dhidi ya Babeli. Atatekeleza mapenzi ya Yahwe dhidi ya Wakaldayo

Hapa "mshirika" ina maana ya Koreshi. Sentensi hizi mbili zina maana moja na zinatumika kwa ajili ya msisitizo.

kusudi lake

"kusudi la Yahwe"

Mimi, mimi

Neno "Mimi" linarudiwa kwa ajili ya msisitizo. "Mimi mwenyewe"

Isaiah 48:16

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Sijazungumza kwa siri

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya chanya. "Nimezungumza dhahiri na wazi"

amenituma

Hapa "mimi" ina maana ya mtumishi asiyejulikana wa Yahwe, huenda Isaya au Koreshi au Masihi alyeahidiwa.

Isaiah 48:17

Mkombozi wako ... Mungu wako

Hapa "wako" ina maana ya watu wa Israeli.

Mkombozi

Mkombozi wa Israeli.

Mtakatifu wa Israeli

Mtakatifu wa Israeli.

ambaye anakuongoza katika njia unayopaswa kuenenda

Yahwe kufundisha watu jinsi ya kuishi inazungumziwa kana kwamba alikuwa akiwaongoza kutembea katika njia sahihi.

Kama tu ungetii amri zangu

Yahwev anafafanua kitu ambacho kingeweza kutokea lakini hakikutokea.

Kisha amani yako na mafanikio yako yangetiririka kama mto, na wokovu yako kama mawimbi ya bahari

Misemo hii miwili inatumia maana moja. Kwazote, Yahwe anazungumzia Israeli kupitia baraka nyingi kana kwamba baraka hizo zilitiririka kama maji.

wokovu yako kama mawimbi ya bahari

Kitenzi kinaweza kutumika kutoka katika msemo uliopita. "wokovu wako ungeweza kutiririka kama mawimbi ya bahari"

Isaiah 48:19

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kufafanua hali ya kubuni kwa watu wa Israeli.

Vizazi vyako viingekuwa vingi kama mchanga, na watoto kutoka tumboni mwako wengi kama punje za mchanga

Zote hizi mbili zina maana ya watu wangekuwa na uzao mwingi zaidi kuliko ya uwezo wao kuhesabu.

watoto kutoka tumboni mwako

Yahwe anazungumzia vizazi vya watu wa Israeli kana kwamba walikuwa watoto ambao taifa liliwazaa.

jina lao halingekatwa mbali wala kufutwa

Watu wa Israeli kuangamizwa inazungumziwa kana kwamba jina lao limekatwa, kama vile mtu anavyokata kipande cha nguo au kukata tawi kutoka katika mti, au kufutwa. Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda.

jina lao

Hapa neno "jina" lina maana ya vizazi ambavyo vingeendelea kubeba jina la Israeli.

halingekatwa mbali wala kufutwa

Misemo hii miwili katikamuktadha hii ina maana ya kuangamiza watu. "kuangamizwa"

Isaiah 48:20

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

hadi kwenye mipaka ya dunia

Sehemu za dunia ambazo zipo mbali sana zinazungumziwa kana kwamba zilikuwa sehemu ambapo dunia hufikia mwisho. Msemo huu pia huunda neno la kujumuisha maneno mengine na lina maana ya kila seheu katikati ya mipaka. "katika sehemu za mbali kabiisa za dunia" au "katika dunia yote"

mtumishi wake Yakobo

Hii ina maana ya vizazi vya Yakobo. "watu wa Israeli, watumishi wake"

Isaiah 48:21

Hawakupata kiu ...maji yalimwagiika nje

Hii ina maana ya tukio katika historia ya watu wa Israeli pale Yahwe alipowatunza walipokuwa wakiishi jangwani baada ya kutoroka Misri.

Isaiah 49

Isaiah 49:1

Nisikilize mimi

Hapa "mimi" ina maana ya mtumishi wa Yahwe.

nyie nchi za pwani

Hii ina maana ya watu ambao huishi katika nchi za pwani. "wewe ambaye mnaishi katika nchi za pwani"

Amefanya mdomo wangu kama upanga mkali

Hapa neno "mdomo" unawakilisha maneno ambayo anazungumza. Maneno yake yanalinganishwa na upanga mkali kusisitiza ya kwamba yatakuwa yanafaa. "Amefanya maneno yangu kuwa na matokeo yanyofaa kuwa makali kama upanga"

amenificha katika kivuli cha mkono wake

Yahwe kulinda mtumishi wake na kuweka kusudi lake kuwa siri inazungumziwa kana kwamba mkono wa Yahwe uliiweka kivuli juu yake.

amenifanya kuwa mshale uliong'arishwa; katika podo lake amenificha

Mtumishi wa Yahwe kuweza kutekeleza makusudi ya Yahwe kikamilifu inazungumziwa kana kwmba mtumishi alikuwa mshale mkali, na mpya.

katika podo lake amenificha

Yahwe kulinda mtumishi wake na kuweka kusudi lake kuwa siri inazungumziwa kana kwamba Yahwe alimficha katika podo.

podo

mfuko unaotumika kubeba mishale

Isaiah 49:3

Taarifa ya Jumla

Mtumishi wa Yahwe anaendelea kuzungumza.

Alisema

"Yahwe alisema"

Wewe ni mtumishi wangu, Israeli

"Wewe ni mtumishi wangu, ambaye ninakuita Israeli"

Isaiah 49:5

Taarifa ya Jumla

Mtumishi wa Yahwe anaendelea kuzungumza.

kwamba Israeli aweze kukusanywa kwake

Sehemu hii ya sentensi ina maana moja na sehemu kabla yake. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "kuleta watu wa Israeli kwake mwenyewe"

Nimeinuliwa katika macho ya Yahwe

Hapa "macho" yanawakilisha mawazo ya Yahwe au fikra. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe ameniinua"

Mungu wangu amekuwa nguvu yangu

Mungu kumpa mtumishi nguvu inazungumziwa kana kwamba Mungu mwenyewe alikuwa nguvu yake. "Mungu wangu amenipa nguvu" au "Mungu wangu ameniimarisha"

nitakufanya kuwa mwanga kwa watu wa mataifa

Mtumishi kuleta ujumbe wa Yahwe kwa watu wa mataifa na kuwasaidia kuelewa inazungumziwa kana kwamba Yahwe alimfanya mtumishi mwanga ambao hung'aa katika watu wa mataifa.

mpaka mwisho wa dunia

Sehemu juu ya dunia ambazo zipo mbali sana zinazungumziwa kana kwamba zilikuwa sehemu ambapo dunia hufika mwisho. Msemo huu pia huunda neno lenye maana moja na kundi la vitu kumaanisha kila sehemu katikati ya mwisho. "katika sehemu zote za mbali za dunia" au "katika dunia nzima"

Isaiah 49:7

Mkombozi

Mkombozi wa Israeli

kwa yule ambaye maisha yake yanadharauliwa, anayechukiwa na mataifa, na mtumwa wa watawala

Hapa neno "maisha" linawakilisha mtu. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "kwa yule ambaye watu walidharau, ambaye mataifa walichukia na kuwashika kama watumwa"

Mtakatifu wa Israeli

Mtakatifu wa Israeli

Isaiah 49:8

Katika kipindi ntakapoamua kuonyesha fadhila yangu nitakujibu, na katika siku ya wokovu nitakusaidia

Vishazi hivi viwili vina maana moja.

nitakujibu

Hapa "nitakujibu" ina maana ya mtumishi wa Yahwe.

katika siku ya wokovu

Hapa neno "siku" ina maana ya muda bayana na sio siku ya masaa 24. Neno "wokovu" linaweza kutafsiriwa kama kitenzi. "pale kipindi kitakapokuja kwangu kukuokoa"

kukupatia kama agano kwa ajili ya watu

Hapa neno "agano" ni mfano wa maneno kwa yule ambaye huanzisha au kupatanisha agano. "kukufanya kuwa mpatanishi wa agano na watu"

kuijenga tena nchi

Hapa neno "nchi" inawakilisha miji katika nchi ambayo ilikuwa imeangamizwa. "kujenga tena sehemu zilizoharibiwa katika nchi"

kugawia tena urithi uliotelekezwa

Yahwe anazungumzia nchi kana kwamba ilikuwa urithi ambao watu wa Israeli walipokea kama milki ya milele. Inadokezwa ya kwamba mtumishi atagawa tena nchi kwa watu wa Israeli. "kugawa tena nchi iliyotelekezwa kama urithi wao"

Isaiah 49:9

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na mtumishi wake.

Watachunga katika barabara, na katika miteremko ya wazi itakuwa malisho yao

Yahwe anazungumzia watu kuishii kwa uhuru na kwa mafanikio kana kwmba walikuwa kondoo ambao walikuwa na malisho mengi ya kuchunga.

Isaiah 49:10

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza.

Hawatakuwa

Hapa "hawatakuwa" ina maana ya watu wa Mungu.

wala joto au jua kupiga juu yao

Hapa neno "joto" linaelezea neno "jua". Watu kuteseka kutoka na joto la jua inazungumziwa kana kwamba joto liliwapiga. "wala hawatateseka kutokana na joto la jua"

kwa maana yeye ambaye ana rehema juu yao ... atawaongoza

Yahwe anazungumzia mwenyewe katika mtu wa tatu. Anazungumzia kuwalinda watu na kuwatunza kana kwamba alikuwa mchungaji wao. "Mim, yule ambaye ana huruma juu yao ... nitawaongoza"

Nitafanya milima yangu yote kuwa njia, na kufanya njia zangu kuu kuwa usawa

Yahwe anazungumza kuwaongoza watu wake kwa usalama na kuondoa vikwazo kutoka katika njia yao kana kwamba aligeuza milima kuwa njia na kusawazisha njia kuu.

Isaiah 49:12

nchi ya Sinimu

Mahali pa eneo hili haipo wazi, lakini inaweza kumaanisha sehemu ambayo ipo kusini mwa Misri.

Imba, mbingu, na uwe na furaha, dunia; funguka katika kuimba, enyi milima!

Isaya anageuza usikivu wake kutoka kwa watu wa Israeli na kuzungumza kwa mbingu, dunia, na milima kana kwamba ilikuwa watu.

Isaiah 49:14

Lakini Sayunii akasema

Neno "Sayuni" ni jina lingine kwa ajili ya Yerusalemu. Isaya anazungumzia mji kana kwamba ulikuwa mwanamke ambaye hulalamika ya kwamba Yahwe amemsahau.

Je! mwanamke anaweza kumsahau mtoto wake, akinyonya katika titi lake, ili asiwe na huruma kwa mwana aliyemzaa?

Yahwe anatuma swali kuwasaidia watu wake kuelewa ya kwamba hatasahau juu yao au kuacha kuwatunza. "Mwanamke hawezi kusahau kunyonyesha mtoto wake au kuacha kumtunza mwana aliyemzaa"

Isaiah 49:16

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza kwa Sayuni.

Nimeandika jina lako juu ya viganja vyangu

Yahwe anazungumzia uaminifu wake usioyumba kwa Sayuni kana kwamba alikuwa ameandika jina lake juu ya viganja vya mkono wake.

kuta zako zipo mbele yangu muda wote

Yahwe anazungumzia kufikiria daima kuhusu Sayuni kana kwamba kuta zake zilikuwa mbele yake daima. Neno "kuta" ni mfano wa maneno kwa ajili ya mji. "Ninaendelea kuwaza juu ya kuta zako" au "Ninakuwaza daima"

Watoto wako wanaharakisha kurudi

Yahwe anazungumzia watu ambao wanarudi kuishi Yerusalemu kana kwamba walikuwa watoto wa mji. "Wakazi wako wanaharakisha kurudi"

Kwa uhakika ninavyoishi

Hiki ni kiapo ambacho Yahwe anatumia kuhakikisha ukweli wa kile anachosema.

tamko la Yahwe

Hii inaweza kuandikwa ili kwamba nomino dhahania "tamko" lielezwa kama kitenzi "tamka" au "sema kwa dhati". "hivi ndivyo Yahwe wa majeshi alivyotamka" au "hivi ndivyo kile Yahwe wa majeshi alivyosema kwa dhati"

hakika utawavaa kama mapambo ya vito; utawaweka juu yako, kama bibi harusi

Yahwe anazungumzia wakazi wa Sayuni kana kwamba walikuwa mapambo ya viito ambayo mji huvaa kuonyesha uzuri wake na furaha.

utawaweka juu yako, kama bibi harusi

Sehemu ya mwisho ya msemo inaweza kubainishwa kutoka katika mstari uliopita. " utawaweka juu yako, kama bibi harusi anavyovaa mapambo ya vito"

Isaiah 49:19

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na Sayuni kana kwamba ilikuwa mwanamke

Ingawa ulikuwa takataka na uliyetelekezwa

Maneno "takataka" na "telekezwa" ina maana moja na inasisitiza ya kwamba adui ameangamiza Sayuni na kuiacha tupu. "Ingawa ulikuwa umetelekezwa kabisa"

wale ambao walikumeza

Aui kuangamiza Sayuni inazungumziwa kana kwamba walikuwa wameimeza. "wale ambao walikuangamiza"

Watoto waliozaliwa wakati wa kuondolewa kwako

Yahwe anazungumzia kipindi ambapo watu wa Yerusalemu walikuwa uhamishoni kana kwamba mji ulikuwa umeondolewa watoto wake. Wale mbao walizaliwa wakati watu wakiwa uhamishoni inazungumziw kana kwamba ni watoto wa mji. "Wale mbao wataishi kwako, ambao walizaliwa wakati watu wakiwa katika uhamisho"

Sehemu ina nafasi ndogo mno kwetu

Hii ina maana ya kwamba ktakuwa na watu wengi sana mpaka mji utakuwa mdogo sana kwa ajili yao wote kuish ndani yake.

Isaiah 49:21

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na Sayuni kana kwamba ilikuwa mwanamke.

Nani amezaa watoto hawa kwa ajili yangu?

Sayuni anazungumza na watu ambao wanrudi kuishi katika mji kana kwamba watu hao walikuwa watoto wake. Swali la Sayuni linaelezea mshangao wake ya kwamba watoto wengi sana sasa ni wa kwake.

Nilondolewa na kuwa tasa, nikahamishwa na kuachwa

Sayuni anajifafanua kama mwanamke asiyeweza kupata watoto zaidi. Anadokeza sababu ya mshangao wake mkubwa.

Nilondolewa na kuwa tasa

"Nilikuwa nikiomboleza juu ya watoto wangu waliokufa na kutoweza kupata wengine"

nikahamishwa na kuachwa

"Niliondoka, bila mume"

Nani amekuza watoto hawa? Tazama, niliachwa peke yangu; hawa wametoka wapi?

Tena, Sayuni anatumia maswali kuelezea mshangao wake. "Tazama, niliachwa peke yangu; sasa watoto hawa wote ambao sikuwakuza wamekuja kwangu"

Isaiah 49:22

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na Sayuni kana kwamba ilikuwa mwanamke. Anafafanua jinsi atakavyoweza kupata watoto wengi sana.

Nitainua mkono wanu kwa mataifa; nitainua bendera yangu ya ishara kwa watu

Vishazi hivi viwili vina maana moja. "Nitainua mkono wangu na kutoa ishara kwa bendera kwa ajili ya watu wa mataifa kuja"

Wataleta wana wako katika mikono yao na kubeba binti zako juu ya mabega yao

Yahwe anazungumzia watu ambao wataishi Yerusalemu kana kwamba walikuwa watoto wa mji. Pia anazungumza kuhusu watu wa mataifa mengine kuwasaidia Waisraeli kurud Yerusalemu kana kwamba walikuwa wakiwabeba Waisraeli.

Isaiah 49:23

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na Sayuni kana kwamba ilikuwa mwanamke.

Wafalme watakuwa baba zako wa kambo, na malkia wao yaya wako

Yahwe anazungumzia watu ambao wataishi Sayuni kana kwamba walikuwa watoto wa mji. Misemo "baba wa kambo" na "yaya" ina maana y wanamume na wanawake ambao huwajibika kwa utunzaji wa watoto. "Wafalme na malkia wa mataifa mengine watajitoa kwa ajili ya wakazi wako"

watainama chini kwako kwa nyuso zao ardhini na kulamba vumbi la miguu yako

Misemo hii inaelezea ishara ambayo watu walitumia kuelezea kujiweka chini kabisa kwa mkubwa zaidi.

kulamba vumbi la miguu yako

Maana zaweza kuwa 1) ya kwamba hii ni ishara halisi ya kujiweka chini ambapo mtu hulamba vumbi kutoka katika mguu wa mkubwa wake au kutoka ardhini katika mguu wa mkubwa wake au 2) ya kwamba hii ni lahaja ambayo inaelezea mtu kusujudu mbele ya mkubwa wake.

hawataaibishwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "hataaibika" au "hatavunjwa matumaini"

Isaiah 49:24

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na Sayuni kana kwamba ilikuwa mwanamke.

Je! mali iliyoibiwa inaweza kuchukuliwa kutoka kwa hodari, au mateka kuokolewa kutoka kwa jeshi kali?

Isaya anatumia swali kuelezea ugumu wa kuchukua kitu chochote kutoka kwa mwanajeshi mwenye uwezo au hodari mwenye nguvu sana. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Mtu hawezi kuchukua mali iliyoibiwa kutoka kwa hodari au kuokoa mateka kutoka kwa wanajeshi wakali"

mali iliyoibiwa

vitu vya thamani vilivyochukuliwa kutoka kwa walioshindwa katika vita.

mateka watachukuliiwa mbali kutoka kwa hodari, na mali iliyoibiwa itaokolewa

Yahwe anasema ya kwamba atafanya kile ambacho kawaida hakiwezekani kwa watu kufanya. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Nitachukua mateka kutoka kwa hodari, na nitaokoa mali iliyoibiwa"

Nita ... kuokoa watoto wako

Yahwe anazungumzia watu ambao wataishi Sayuni kana kwamba walikuwa watoto wa mji.

Isaiah 49:26

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na Sayuni kana kwamba ilikuwa mtu.

Nitawalisha wakandamizaji wako kwa nyama yao wenyewe

Maana zaweza kuwaa 1) wakandamizaji watakuwa na njaa sana watakula nyama ya rafiki zao waliokufa. "Nitasababisha wakandamizaji wako kula nyama yao wenyewe" au 2) Yahwe anazungumzia wakandamizaji kupigana dhidi yao wenyewe na kujiangamiza kana kwamba walikuwa wakijila wenyewe. "Nitasababisha wakandamizaji wako kujiangamiza wao wenyewe, kana kwamba walikuwa wakila nyama yao wenyewe"

na watalewa katika damu yao wenyewe, kan kwamba ilikuwa divai

Maana zaweza kuwa 1) wakandamizaji watakuwa na kiu sana mpaka watakunywa damu ya rafiki zao ambao wamekufa. "na watakunywa damu ya rafiki zao na kuwa kama watu dhaifu waliolewa divai" au 2) Yahwe anazungumzia wakandamizaji kupigana dhidi yao wenyewe na kujiangamiza kana kwamba walikuwa wakinywa damu ayo wenyewe. "na watamwaga damu nyingi sana ya rafiki zao kana kwamba walikuwa wakilewa na divai"

Isaiah 50

Isaiah 50:1

Hati ya talaka ambayo nilimuacha mama yako iko wapi?

Yahwe anazungumza juu ya Sayuni kana kwamba mji ulikuwa mama wa watu walioishi kule na kutuma watu katika uhamisho kana kwamba alikuwa akitoa talaka kwa mama yao.

Hati ya talaka ambayo nilimuacha mama yako iko wapi?

Yahwe anauliza swali hili la balagha ili kwamba watu watoa "hati ya talaka" ambayo ingetoa sababu ya Yahwe kuwatuma katika uhamisho. "Nionyesheni hati ya talaka mabyo nilimuacha mama yenu"

Ni wadai wapi wa kwangu nimekuuza?

Yahwe anazungumzia kuwafukuza watu katika uhamisho kana kwamba alikuwa akiwauza.

Ni wadai wapi wa kwangu nimekuuza?

Yahwe anauliza swali hili kusisitiza ya kwamba hakuwauza kwa sababu alikuwa na deni kwa mdaiwa. Inadokezwa ya kwamba hiki ndicho watu walivyofikiri. "Sikuwauza kwa sababu ninadaiwa na mtu"

uliuzwa kwa sababu ya dhambi zako, na kwa sababu ya uasi wako, mama yako alifukuzwa

Yahwe anatoa sababu ya kuwafukuza watu katika uhamisho, ambayo anazungumzia kana kwamba amewauza na kutengana na mama yao. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Nilikuuza kwa sababu ya dhambi zako, na nikatengana na mama yako kwa sababu ya uasi wako"

Isaiah 50:2

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzunguza na watu wa Israeli.

Kwa nini nilikuja lakini hapakuwa na mtu kule? Kwa nini niliita lakini hakuna aliyejibu?

Sentensi hizi mbili kimsingi zina maana moja. Yahwe anatumia maswali kusisitiza ya kwamba watu wapo uhamishoni kwa sababu hawakuitikia kwake, sio kwa sababu hakuwa tayari kuwaokoa. "Nilipokuja kwako, ulipaswa kuwa pale, lakini haukuwepo. Nilipokuita, ulitakiwa kujibu, lakini haukujibu". au "Nilipokuja kuzungumza na wewe, haukuniitikia".

Je! mkono wangu ulikuwa mfupi sana kukukomboa? Je! hapakuwa na nguvu ndani mwangu kukuokoa?

Yahwe anatumia maswali mawili ya kufanana kukaripia watu kwa kuamini ya kwamba hakuwa na nguvu ya kutosha kuwaokoa. "Mkono wangu hakika haukuwa mfupi kwangu kukulipia, na nilikuwa na uwezo kukuokoa!" au "Hakika nina uwezo wa kuwaokoa kutoka kwa adui wako"

Je! mkono wangu ulikuwa mfupi sana

Hapa neno "mkono" unawakilisha nguvu ya Yahwe. Yahwe kutokuwa na nguvu ya kutosha inazungumziwa kana kwamba mkono wake ulikuwa mfupi. "Je! sikuwa na nguvu ya kutosha"

Je! hapakuwa na nguvu ndani mwangu

"Je! sikuwa na nguvu"

naifanya mito kuwa jangwa

Yahwe anazungumzia kukausha mito kana kwamba alikuwa akigeuza kuwa jangwa. "Ninafanya mito kukauka kama jangwa"

samaki wao hufa kwa kukosa maji na kuoza

"samaki wao hufa na kuoza kwa kukosa maji". Neno "wao" ina maana ya bahari na mito.

naivisha mbingu kwa giza; naifunika kwa nguo ya gunia

Misemo hii miwili kimsingi ina maana moja. Yahwe inazungumza kusababisha mbingu kuwa na giza kana kwamba alikuwa akiivika kwa nguo ya gunia. "Ninafanya mbingu kuwa giza, kana kwamba ilikuwa ikivaa nguo nyeusi ya gunia"

Isaiah 50:4

Taarifa ya Jumla

mtumishi wa Yahwe anaanza kuzungumza.

Bwana Yahwe amenipatia ulimi kama wale wanaofundishwa

Neno "ulimi" linawakilisha kile anachosema. Maana zaweza kuwa 1) Yahwe amemwezesha kuzungumza kama mtu ambaye amejifunza kuzungumza kwa ustadi. "Bwana Yahwe ameniwezesha kuwa msemaji mwenye ujuzi" au 2) Yahwe kanifundisha kile nachosema. "Bwana Yahwe ameniwezesha kuzungumza kile alichonifundisha"

anaamsha sikio langu kusikia

Hapa "sikio langu" ina maana ya mtumishi wa Yahwe. Yahwe kumwezesha kusikia na kuelewa kile ambacho Yahwe anafundisha inazungumziwa kana kwamba Yahwe aliamsha sikio lake kutoka usingizini. "ameniwezesha kuelewa kile anachosema"

kama wale wanaofundishwa

Mtumishi anajilinganisha na mwanafunzi ambaye hujifunza kutoka kwa mwalimu wake. Maana zawekana kuwa 1) "kama mtu ambaye hujifunza kutoka kwa mwalimu wake" au 2) "kama mtu ambaye amemfundisha"

Isaiah 50:5

Taarifa ya Jumla

Mtumishi wa Yahwe anaendelea kuzungumza.

Bwana Yahwe amefungua sikio langu

Yahwe kumwezesha mtumishi wake kusikia na kuelewa inazungumziwa kana kwamba Yahwe alifungua sikio lake. "Bwana Yahwe ameniwezesha kumsikia na kumwelewa"

na sikuwa muasi, wala sikugeuka kinyume

Misemo hii miwili kimsingi ina maana moja. Kutotii kile ambacho Yahwe alisema inazungumzwa kana kwamba ilikuwa kugeuza mgongo wa mtu kwake. Hii inaweza kuelezwa katika misemo chanya. "na nikatii kile alichosema"

Niliwapa mgongo wale walionipiga, na mashavu yangu kwa wale walionyofoa ndevu zangu

Kuruhusu watu kumpiga na kunyofoa ndevu zake inazungumziwa kana kwamba ilikuuwa kutoa mgongo wake na mashavu kwao. "Niliruhusu watu kunipiga mgongoni na kunyofoa ndevu zangu kutoka mashavuni mwangu"

Sikuficha uso wangu kutoka kwa matendo ya aibu na kutemewa

Kuficha uso wa mtu ina maana ya kujilinda. "Sikujihami pale waliponidhihaki na kunitemea"

Isaiah 50:7

Taarifa ya Jumla

Mtumishi wa Yahwe anaendelea kuzungumza.

kwa hiyo sijaaibika

Ingawa mtumishi ametendewa vibaya, hataaibika kwa sababu amemtii Yahwe. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "kwa hiyo sitaaibika"

kwa hiyo nimefanya uso wangu kama jiwe gumu

Hapa "uso wangu" una maana ya mtumishi. Mtumishi kuwa na nia imara ya kumtii Yahwe inazungumziwa kana kwamba uso wake ulikuwa mgumu kama jiwe. "kwa hiyo nina nia dhahiri"

kwa maana najua sitapatwa na aibu

Mtumishi huyu anatazama muda ujao kwa uhakika, salama katika wito wa Yahwe. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "kwa maana najua ya kwamba maadui wangu hawataweza kunifanya nihisi aibu"

Isaiah 50:8

Taarifa ya Jumla

Mtumishi wa Yahwe anaendelea kuzungumza.

Nani atakayenipinga? Tusimame ... Nani mshtaki wangu? Na aje

Mtumishi anatumia maswali haya kusisitiza uya kwamba hakuna mtu ambaye anaweza kumshtaki kwa haki kwa ubaya. "Kama mtu yeyote anaweza kunipinga, tusimame ... Kama mtu yeyote atanipinga, na aje"

Nani atanitamka kuwa na hatia?

Mtumishi anatumia swali hili kuweka uzito ya kwamba hakuna mtu wa kumtamka kuwa na hatia. "Hakuna mtu yeyote ambaye anaweza kunitamka kuwa na hatia"

watachakaa kama nguo; nondo utawala

Kule ktokuwa na mtu aliyesalia kumshtaki mtumishi kwa kuwa na hatia inazungumziwa kana kwamba washtaki walikuwa nguo ambazo hupwaya na huliwa na nondo.

Isaiah 50:10

Taarifa ya Jumla

Mtumishi anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Ni nani miongoni mwenu anamwogopa Yahwe? Ni nani anayetii sauti ya mtumishi wake? Ni nani anayetembea katika giza zito bila nuru? Anatakiwa ... Mungu wake.

Mtumishi anatumia maswali haya kuwatambua wale ambao anazugumza nao. "Kama mtu miongoni mwenu anamwogopa Yahwe na kutii sauti ya mtumishi wake, lakini anatembea katika giza zito bila nuru, basi anatakiwa ... Mungu wake"

anayetii sauti ya mtumishi wake

Hapa neno "sauti" linawakilisha kile mtumishiu anachosema. "kumtii mtumishi wake"

anayetembea katika giza zito bila nuru

Mtumishi anazungumzia watu ambao wanateseka na kuhisi kutojiweza kana kwamba walikuwa wakitembea katika sehemu ya giza sana. "anateseka na anajihisi kutojiweza"

tumaini katika jina la Yahwe na mtegemee Mungu wake

Misemo hii miwili kimsingi ina maana moja. Hapa neno "jina" linawakilisha Yahwe mwenyewe. Kumtumaini Mungu inazungumziwa kana kwamba ilikuwa kumuegemea yeye. "mtumaini Yahwe, Mungu wake"

Isaiah 50:11

nyie wote mnaowasha moto ... miale ambayo umeiwasha

Hii inaendeleza sitiari kutoka kwa mstari wa nyuma wa watu ambao hutembea gizani. Hapa watu wanaojaribu kuishi kulingana na hekima yao badala ya kumtumaini Bwana wanazungumziwa kana kwamba wamewasha moto wao na kubeba tochi ili kuona gizani.

utalala chini katika nafasi ya maumivu

Hapa "kulala chini" ina maana ya kufa. Kufa kwa maumivu inazungumziwa kana kwamba ilikuwa kulala chini katika nafasi ambayo watapitia maumivu. "utakufa kwa mateso makubwa"

Isaiah 51

Isaiah 51:1

Nisikilizeni mimi

Hapa neno "mimi" lina maana ya Yahwe.

Utazameni mwamba ... na kwa machimbo

Kutazama kitu inawakilisha kufikiria juu yake. "ninafikiria juu ya mwamba ... na machimbo"

mwamba ambao ulichongwa na kwa machimbo ambayo ulikatwa

Mungu anazungumza kuhusu taifa la Israeli kana kwamba lilikuwa jengo lililotengenezwa kwa mawe kana kwamba mababu zao walikuwa mwamba au machimbo ambayo Mungu aliwakata. Hi inaweza kuwekwa wazi. "mababu zako, ambao n kama mwamba ambao ulichongwa na machimbo ambayo ulikatwa"

mwamba ambao ulichongwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "mwamba ambao nilikuchonga"

ulichongwa

"kukata kwa patasi" au "kukata"

machimbo ambayo ulikatwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "machimbo ambako nimekukata"

Isaiah 51:2

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Abrahamu, baba yako

Mungu anazungumzia mababu zao kana kwamba alikuwa baba yao. "Abrahamu, babu yako" au "Abrahamu, mhenga wako"

Sara, aliyekuzaa

Mungu anazungumzia mke wa Abrahamu kana kwamba alikuwa mama yao na amewazaa wao. "Mke wa Abrahamu, Sara, ambao nyote ni vizazi vyake"

alipokuwa mtu binafsi

Hii ina maana pale alipokuwa bado hana watoto. Hii inaweza kuwekwa wazi. "alipokuwa hana watoto"

kumfanya kuwa wingi

Mungu anazungumzia uzao wa Abrahamu kuwa wengi kana kwamba Abrahamu alikuwa wingi. "alifanya uzao wake kuwa wengi" au "alimfanya kuwa na uzao mwingi"

Isaiah 51:3

Yahwe atafariji Sayuni

Mji wa Sayuni, ambao unaitwa Yerusalemu, hapa unawakilisha watu wa Sayuni. "Yahwe atafariji watu wa Sayuni"

atafariji maeneo yake yote yasiofaa

"atafarijii watu ambao wanashi katika maeneo yake yote yasiyofaa"

maeneo yake yasiofaa ... nyika zake ... jangwa lake tambarare

Neno "yake" ina maana ya Sayuni. Miji mara nyingi huzungumziwa kana kwamba ilikuwa wanawake.

maeneo yasiofaa

sehemu ambazo imeangamizwa

nyika yake alifanya kama Edeni, na jangwa lake tambarare ... kama bustani ya Yahwe

Misemo hii ina maana ya kwamba Mungu atafanya maeneno tupu ya israeli mazuri. Katika unabii, matukio ambayo yatatokea katika siku za usoni mara nyingi kufafanuliwa kama kuwa kipindi cha nyuma. Hii inasisitiza ya kwamba hakika yatatokea. "atafanya nyika zake kama Edeni na jangwa zake tambarare ... kama bustnai ya Yahwe.

shangwe na furaha zitapatikana ndani yake

Shangwe na furaha ina maana moja. Kukutwa kule ina maana ya kuwa kule. "kutakuwa na shangwe na furaha Sayuni tena"

Isaiah 51:4

Maelezo ya Jumla

Yahwe anazungumza na watu wa Israeli.

Kuwa msikivu kwangu ... nisikilizeni mimi

Misemo hii miwili ina maana moja. Kwa pamoja inaimarisha amri ya kusikiliza.

Nitafanya haki yangu kuwa mwanga kwa ajili ya mataifa

Hapa haki ya Mungu inawakilisha sheria yake, na mwanga unawakilisha maarifa ya kilicho sahihi. Hii ina maana watu wa mataifa wataelewa na kutii sheria ya Mungu. "sheria yangu utafundisha mataifa kilicho sahihi" au "mataifa watajua sheria yangu"

Haki yangu ipo karibu

Wazo la "karibu" inawakilisha "hivi karibuni". Haki ya Mung kuwa karibu inawakilisha yeye kuonyesha haki yake hivi karibuni. Atafanya hivi kwa kutimiza ahadi zake na kukomboa watu. "Hivi punde nitaonyesha haki yangu"

wokovu wangu utatoka nje

Mungu anazungumzia kuwaokoa watu kana kwamba wokovu wake ulikuwa kitu ambacho kinaweza kutoka nje kwao. "Nitaokoka watu"

mkono wangu utahukumu matafa

Hapa mkono wa Mungu unawakilisha nguvu yake, na kuhukumu inawakilisha utawala. "Nitatawala mataifa kwa nguvu yangu"

pwani

Hii ina maana ya watu ambao wanaishi katika pwani ya nchi za mbali kupita bahari. "watu amboo wanashi katika pwani" au "watu ambao wanaishi katiak nchi kupita bahari"

watasubiri kwa shauku kwa ajili ya mkono wangu

Hapa mkono wa Mungu unawakilisha kile atakachofanya. Hapa ina maana ya yeye kokoa watu. "watasubiri kwa shauku kwangu kufanya kitu" au "watanisubiri kwa shauku niwaokoe"

Isaiah 51:6

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Inua macho yako mbinguni

Kuinua macho inawakilisha kutazama kitu kilicho juu. "Tazama juu angani"

kama moshi ... kama vazi ... kama nzi

Zote hizi zina maana ya vitu ambavyo hutoweka kwa haraka na kirahisi au kutokuwa na thamani.

wokovu wangu utaendelea milele

"wokovu" wa Mungu hapa unawakilisha matokeo ya wokovu wake, ambayo ni uhuru. "Nitakuokoa, utakuwa huru milele"

haki yangu haitakoma kutumika

"haki" ya Mungu hapa inawakilisha yeye kutawala kwa haki. "utawala wangu wa haki hautakuwa na mwisho" au "nitatawala kwa haki milele"

Isaiah 51:7

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

ambao mna sheria yangu mioyoni mwenu

Kuwa na sheria ya Mungu moyoni inawakilisha kujua sheria ya Mungu na kutaka kuitii. "ambaye anajua na kuinua sheria yangu"

wala msivunjwe mioyo kwa matusi yao

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "na usipoteze ujasiri wako watakapokuumiza"

Kwa maana nondo watawala kama vazi, na funza watawala kama sufu

Mungu anazungumzia watu kutukana wale ambao wana haki kana kwamba walikuwa mavazi ya sufu, na kuangamizwa kwao kana kwamba wadudu waliwala.

haki yangu itakuwa milele

"haki" ya Mungu hapa inawakilisha yeye kutawala kwa haki. "utawala wangu wa haki hautakuwa na mwisho" au "nitatawala kwa haki milele"

na wokovu wangu kwa vizazi vyote

"wokovu" wa Mungu hapa unawakilisha matokeo ya wokovu wake, ambayo ni uhuru. Kuwa "kwa vizazi vyote" inawakilisha kudumu milele. "Nitakuokoa, na utakuwa huru milele"

Isaiah 51:9

Amka, amka, jivike kwa nguvu, mkono wa Yahwe

Watu huuliza kwa haraka kwa mkono wa Yahwe kuwasaidia kana kwamba mkono wake ulikuwa mtu. Kama haiwi ajabu kuzungumza kwa mkono, hii inaweza kuwekwa moja kwa moja kwa Yahwe badala yake. "Amka, amka, Yahwe, na jivike mkono wako kwa nguvu"

Amka, amka ... mkono wa Yahwe

Watu wanazungumza kana kwamba mkono wa Yahwe ulikuwa umelala kwa sababu haukuwa unawasaidia. Wanautakaa uwasaidie. Neno "amka" linarudiwa kuonyesha ya kwamba wanahtaji msaada wa Mungu haraka.

jivike kwa nguvu

Nguvu inazungumziwa kana kwamba ilikuwa aina ya nguo ambayo watu walivaa kujiimarisha vitani. "jiweke uwe na nguvu"

Je! sio wewe uliyemponda jitu wa baharini, wewe uliyemchoma joka?

Msemaji anatumia swali kusisitiza nguvu ya Yahwe kufanya mambo makuu. "Ni wewe ambaye ulimponda jtu wa bahari, wewe ambaye alimchoma joka"

jitu wa bahari ... joka

Zote hizi zina maana moja. Zina maana ya Rahabu, nyoka wa kimithiolojia ambaye anaishi baharini, ambayo inaweza kuashiria taifa la Misri au kuashiria uovu na machafuko.

Je! si wewe uliyekausha bahari ... kwa ajili ya waliokombolewa kupita katikati?

Tena, msemaji anatumia maswali kusisitiza nguvu ya Yahwe kufanya mambo makuu. Hii ina maan Yahwe kufungua Bahari ya Shamu kwa Waisraeli kuvuka na kutoroka jeshi la Misri. "Ulikausha bahari ... kwa ajili ya waliokombolewa kupita katikati".

Isaiah 51:11

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Waliokombolewa wa Yahwe

"kukomboa" ina maana ya "kuokoa". Hii ina maana ya watu ambao Yahwe aliwaokoa. "Wale ambao Yahwe aliwaokoa"

kwa furaha milele juu ya vichwa vyao

Hii inatumia kichwa cha mtu kumaansha mtu kwa ukamilifu. "watakuwa na furaha milele"

furaha na shangwe ... huzuni na majonzi

Maneno "shangwe" na "furaha" yana maana moja, kama vile "huzuni" na "majonzi". Kwa pamoja yanasisitiza ukali wa hisia hizi.

furaha na shangwe zitawapita

Hii inazungumzia watu kuzidiwa na furaha na shangwe kwa kuzipatia hisia hizi sifa za binadamu za kuwa na uwezo wa kumpita mtu. "watazidiwa kabisa na shangwe na furaha" au "watakuwa na furaha na shangwe kabisa"

huzuni na maombolezo zitatoweka

Hii inazungumzia watu kutokuw na huzuni na majonzi tena kwa kuzungumza juu ya hisia hizi kana kwamba zinaweza kutoroka. "hawatakuwa na huzuni na maombolezo tena"

Isaiah 51:12

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Mimi, mimi, ndiye yeye

Neno "Mimi" inarudiwa kwa msisitizo.

Kwa nini unawaogopa wanadamu ... kama nyasi?

Swali hili la balagha linasisitiza ya kwamba watu ambao wana ulinzi wa Mungu wanatakiwa kutowaogopa wanadamu. Hii inaweza kuandikwa kama kauli. "Usiogope wanadamu ... kama nyasi"

ambao wametengezwa kama nyasi

Msemo huu unalinganisha wanamume na nyasi kusisitiza ya kwamba maisha yao ni mafupi na kwamba wanakufa upesi. "ambao wanaishi na kufa haraka kama nyasi" au "ambao watanyauka na kutoweka kama nyasi"

ambao wametengezwa kama

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "ambao ni kama"

Isaiah 51:13

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Kwa nini mmemsahau Yahwe ... dunia?

Yahwe anatumia swali kusisitiza ya kwamba hawatakiwi kumsahau Yahwe. Hii inaweza kuandikwa kama kauli. "Haukutakiwa kuwa umemsahau Yahwe ... dunia"

Muumba

Muumba wa mbingu na nchi

aliyezinyosha mbingu

"aliyeinyosha anga". Hii inazungumzia Yahwe kuumba mbingu kana kwamba alikuwa amenyosha kwa njia moja anavyosha vazi kubwa. "ambaye alinyosha mbingu kama vazi"

misingi ya dunia

Neno "msingi" kawaida lina maana ya maumbo ya mawe ambayo hutoa mhimili kwa jengo kutoka chini. Hapa inafafanua umbo linalofanana ambalo inasadikiwa kuwa mhimili na kushikilia dunia katika nafasi yake.

ghadhabu ya moto ya mkandamizaji anapoamua kuangamiza

"ghadhabu ya moto ya mkandamizaji atakapoamua kusababisha uharibifu"

ghadhabu ya moto

Hapa neno "moto" lina maana ya "imara" au "kuu". "ghadhabu kuu"

Iko wapi ghadhabu ya mkandamizaji?

Yahwe anatumia swali kusisitiza ya kwamba watu wanapaswa kutoogopa wale ambao wanataka kuwakandamiza. Wakandamzaji wao sio tishio kwao tena. Hii inaweza kuandikwa kama kauli. "Ghadhabu ya mkandamizaji sio tishio"

Isaiah 51:14

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Yule ambaye ameinamishwa chini

Hii ina maana ya watu wa Israeli ambao ni watumwa wa Babeli. Msemo huu unafafanua namna wanvyofanya kazi. "Mtumwa"

shimo

Hii ina maana ya Kuzimu. "shimo la kuzimu" au "kaburi"

wala hatapungukiwa mkate

Hapa "mkate" unawakilisha chakula kwa ujumla. Hii inaweza kuandikwa kwa hali ya chanya. "wala atakuwa bila chakula"

ambaye huvurugavuruga bahari

Hii inazungumzia Yahwe kusababisha bahari kusogea na mawimbi kuinuka na kuanguka kana kwamba alikuwa akikoroga bahari kama mtu anavyokoroga ujazo wa bakuli kwa kijiko kikubwa. "ambaye anasababisha bahari kuvurugwa" au "ambaye hufanya bahari kusogea juu na chini"

mawimbi yake yaungurume

Muungurumo ni sauti ya juu ya nguvu unayofanywa na kitu chenye uhai, kama vile dubu au simba. Hapa mawimbi yanaelezwa kama kutengeneza sauti ya nguvu. "mawimbi huanguka kwa sauti"

Yahwe wa majeshi

Yahwe wa majeshi ya Israeli.

Isaiah 51:16

Nimeweka maneno yangu kinywani mwako

Hii inazungumzia Yahwe kumwambia Isaya anachotakiwa kusema kana kwamba maneno yake yalikuwa chombo halisi. Yahwe aliweka kinywani mwa Isaya. "Nimekwambia nini cha kusema"

Nimekufunika katika kivuli cha mkono wangu

"mkono" wa Yahwe una maana ya nguvu. Hii inazungumzia Yahwe kumlinda Isaya kana kwamba mkono wake ulikuwa umemfunika kumlinda. "nguvu yangu imekuweka salama" au "Nimekulinda na kukuweka salama"

ili kwamba nipande mbingu

Neno "panda" ina maana ya kuimarisha kitu ardhini. Hapa Yahwe kuimarisha mbingu inazungumziwa kana kwamba mbingu ilikuwa hema ambalo lingesambaa na kuwekwa imara kwa kigingi cha hema. "ili niweze kuimarisha mbingu"

kutandaza misingi ya dunia

Neno "msingi" kawaida lina maana ya maumbo ya mawe ambayo hutoa mhimili kwa jengo kutoka chini. Hapa inafafanua umbo linalofanana ambalo inasadikiwa kuwa mhimili na kushikilia dunia katika nafasi yake.

Isaiah 51:17

Amka, amka, simama, Yerusalemu

Hapa "Yerusalemu" inawakilisha watu wanaoishi pale. Yahwe anazungumzia watu wa Yerusalemu kana kwamba walikuwa wakimsikiliza. "Amka, amka, simama, nyie watu wa Yerusalemu"

Amka, amka, simama

"Uwe tayari na inuka". Kurudia kwa neno "amka" linasisitiza uharaka wa wito kuamsha watu wa Israeli. Hautumiki kuwaamsha kutoka usingizi halisi.

wewe ambaye umekunywa kutoka katika mkono wa Yahwe ... kutoka katika kikombe cha kupepesuka

Yahwe anazungumzia kuwaadhibu watu wake kana kwamba alikuwa amewalazimisha kunywa kutoka katika bakuli ambalo lilijazwa na hasira yake. Na walipokunywa bakuli la hasira yake, walipepesuka kana kwamba walikunywa mvinyo mwingi.

chini mpaka kwenye masimbi

Neno "masimbi" lina maan ya vipande vya chini ya chombo ambacho kinywaji kilkuwemo. "mpaka chini kabisa"

kutoka katika mkono wa Yahwe

Hapa Yahwe anamaanishwa kwa mkono wake kusisitiza ya kwamba yeye ndiye aliyetoa bakuli kwa watu wake. "ambayo alikupatia"

katika kikombe cha kupepesuka

"kutoka katika kikombe ambacho kimesababisha upepesuke kana kwamba ulilewa kwa mvinyo"

kupepesuka

kutotembea wiima, au kujikwaa akiwa anatembea

Hakuna mtu ... wa kumuongoza; hakuna mtu ... kumchukua kwa mkono

Vishazi hivi viwili vina maana moja na vinaweza kujumlishwa. Hii inazungumzia Yerusalemu kutojiweza kana kwamba mji uliikuwa mwanamke mlevi bila mtoto wa kumsaidia kutembea kwa usalama. "Hauna mtu wa kukusaidia! Wewe ni kama mwanamke mzee aliyelewa asiye na mwana kumchukua kwa mkono na kumuongoza"

Isaiah 51:19

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

ni nani atasikitika pamoja na wewe? ... Nani atakufariji?

Isaya anatumia maswali kusisitza ya kuwa sasa hakuna mtu wa kulia pamoja nao au kuwafariji. Maswali haya yanweza kuandikwa kama kauli. "lakini hakuna mtu wa kulia pamoja nawe ... Hakuna mtu w kukufariji"

Shida hizi mbili

Shida hizi mbili zina maana ya "ukiwa na uharibifu" na "njaa na upanga".

ukiwa na uharibifu

Maneno haya yana maana moja na husisitiza uharibifu wa nchi unaosababishwa na jeshi pinzani. "adui zako wameacha miji tupu na kuharibiwa"

njaa na upanga

Maneno "njaa" na "upanga" yanafafanua shida ambazo zitakuja juu ya watu. "Upanga" una maan ya "vita". "wengi wenu mmekufa kutokana na njaa na vita"

wanalala katika kila kona ya mtaa

Huu n ujumla, ambayo ina maana ya watoto wengi watalala mitaani, lakini sio katika kila kona ya mtaa. "wanalala mtaani"

kama paa ndani ya wavu

Hii inazungumzia watoto kuchoka sana na kutojiweza kana kwamba walikuwa paa waliokamatwa katika mtego. "hawajiwezi, kama paa aliyeshikwa katika wavu" au "kutojiweza kama paa aliyetegwa"

paa

Huyu ni mnyama, anayefanana na mbawala, ambaye ana pembe na hukimbia haraka sana.

wamejaa hasira ya Yahwe, karipio la Mungu wako

"hasira ya Yahwe" ina maana ya Yahwe kuadhibu watu wake kwa sababu ya hasira yake dhidi yao. Hii inazungumzia watu kuadhibiwa sana kana kwamba wamejaa hasira ya Yahwe. Pia, neno "karipia" linaweza kuandikwa kama kitenzi. "wameahibiwa sanana Yahwe kwa sababu alikuwa na hasira sana kwao na kuwakaripia"

Isaiah 51:21

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

wewe uliyekandamizwa na wewe uliyelewa

Yahwe anatumia neno "uliyekandamizwa" hapa kumaanisha watu wote waliokandamizwa. "nyie watu mliokandamizwa na walevi"

wewe uliyelewa, lakini sio ulevi wa mvinyo

Hii inazungumzia watu kujifanya wamelewa kwa sababu wanateseka kana kwamba wamelewa kwa kulazimishwa kunywa bakuli ya hasira y Yahwe. "wewe ambaye umelewa kwa kunywa mvinyo wa bakuli la hasira ya Yahwe" au "wewe unayejifanya umelewa, kwa sababu umeteseka sana"

Tazama, nimechukua kikombe cha kupepesuka kutoka mkononi mwako - bakuli, ambalo ni kikombe cha hasira yangu - ili kwamba

Hii inazungumzia Yahwe kutokuwa na hasira na watu wake kana kwamba hasira yake likuwa ujazo wa kikombe ambacho alikuwa akikichukua kutoka kwao. "Sitakuwa na hasira na wewe tena. Tazama, ni kana kwamba nimechukua kutoka kwako kikombe kilichokufanya upepesuke, yaani, kikombe ambacho kilijaa hasira yangu, ili kwamba"

Tazama

Hii ni lahaja inayotumika kuvuta nadhari ya msikilizaji kwa kile kinachosemwa baadaye. "sikiliza"

kikombe cha kupepesuka

Neno "kikombe" ina maana ya kile kilicho ndani ya kikombe. "kikombe cha divai ambacho huwafanya watu wapepesuke"

bakuli, ambalo ni kikombe cha hasira yangu

Yahwe anazungumza kuwaadhibu watu kana kwamba aliwalazimisha kunywa kutoka katika bakuli ambalo lilijazwa hasira yake. "bakuli ambalo lilijazwa hasira yangu" au "kikombe ambacho kilijazwa hasira yangu"

Isaiah 51:23

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Nitakiweka katika mkono wa msumbufu wako

Hii inazungumzia Yahwe kuwaadhibu adui zake kana kwamba alikuwa akienda kuwalazimisha kunywa kutoka katika kikombe kilichojaa hasira yake.

Nitakiweka katika mkono wa msumbufu wako

Inadokezwa ya kwamba kwa kuweka kikombe cha hasira yake katika mkono wao Yahwe atakuwa anawalazimisha kunywa kile kilicho katika kikombe. "Nitawalazimisha wasumbufu wako kunywa kutoka katiika mvinyo wa bakuli la hasira yangu"

msumbufu wako

Neno "wasumbufu" inaweza kuelezwa kwa kitenzi. "wale ambao wamekusumbua" au "wale ambao wamekusababisha kuteseka"

ulifanya mgongo wako kama ardhi na kama mitaa kwa ajili yao kutembea juu

Hii inalinganisha namna adui zake walitembea juu ya migongo yao kwa namna watu wanavyotembea juu ya mitaa. "unalala katika mitaa ili maadui zako waweze kutembea juu ya migongo yako"

Isaiah 52

Isaiah 52:1

Amka, amka

Neno hili linarudiwa kwa msisitizo na kuonyesha uharaka. Isaya kujaribu kuamsha watu inazungumziwa kana kwamba alikuwa akijaribu kuwaamsha kutoka usingizini.

vaa nguvu yako

Kuwa na nguvu tena inazungumziwa kana kwamba nguvu ilikuwa mavazi ambayo mtu huvaa. "uwe na nguvu"

Sayuni ... Yerusalemu

Zote hizi zina maana ya watu ambao huishi katika Yerusalemu. Isaya anazungumzia watu kana kwamba walikuwa wakimsikiliza. "watu wa Sayuni ... watu wa Yerusalemu"

asiyetahiriwa au mchafu

Vivumishi vidogo vinaweza kuwekwa kama vivumishi. "Wale ambao hawajatahiriwa au wale ambao sio wasafi"

wachafu

Hii ina maana ya watu wachafu. Mtu ambaye Mungu humchukulia kutokubalika kiroho au kunajisiwa inazungumziwa kana kwamba mtu alikuwa mchafu kimwili. "wale ambao hawakubaliki kwa Mungu"

ataingia kwako

Hapa "kwako" ina maana ya Yerusalemu ambayo inawakilisha watu wanaoishi pale. Inaeleweka ya kwamba wasiotahiriwa na watu wachafu wataingia katika mji kuwashambulia watu. Maneno ambayo hayapo yanaweza kuongezwa kufanya maana wazi. "ingia mji wako kukushambulia"

Isaiah 52:2

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Jikung'ute kutoka mavumbini; amka na ukae, Yerusalemu

Hapa "Yerusalemu" inawakilisha watu wanaoishi kule. "Watu wa Yerusalemu, simama wima na ukung'ute uchafu kutoka kwako"

ondoa mnyororo kutoka shingoni mwako, mfungwa

Inaonyeshwa ya kwamba watu wa Yerusalemu walikuwa wakivaa minyororo kwa sababu walikuwa watumwa walipokuwa uhamishoni Babeli. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi.

binti Sayuni

Hii ni lahaja. "binti" wa mji ina maana watu wa mji ule. "watu wa Sayuni" au "watu ambao wanaishi Sayuni"

Uliuzwa bure, na utakombolewa bila fedha

Hii inazungumzia kuhusu Yahwe kana kwamba alikuwa mmiliki wa watu wa Israeli. Kwa kuwa ni mmiliki halali anaweza kuwatoa au kuwarudisha atakavyotaka. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. :Nimekuuza bure, na nitakukomboa bila fedha"

Isaiah 52:4

Hapo mwanzo

Hapa "mwanzo" ina maana ya mwanzo wa historia ya Israeli walipoanza kuwa watu.

walikwenda chini mpaka Misri

"walikwenda mpaka Misri". Ilikuwa kawaida kutumia msemo "kushuka chini" pale inapozungumziwa kusafiri kutoka Kaanani mpaka Misri.

Ashuru imewakandamiza

Ashuru ina maana ya watu wa Ashuru. "watu wa Ashuru wamewatendea vibaya"

Isaiah 52:5

Basi sasa nina nini hapa ... kuona ya kwamba watu wangu wanachukuliwa bure?

Yahwe anatumia swali kufanya watu kuzingatia kwa makini kile anachotaka kusema. Swali hili la balagha linaweza kutafsiriiwa kama kauli. "Basi sasa tazama kile kinachotokea ... watu wangu wanachukuliwa tena bure"

nina nini hapa - hili ni tamko la Yahwe - kuona

Maana zaweza kuwa 1) Yahwe anasema, "hili ni tamko la Yahwe". "Ninalo hapa - hiki ndicho kile nachotamka- kuona" au 2) Isaya anasema, "Hili ni tamko la Yahwe". "Ninalo hapa, anatamka Yahwe, "kuona"

kuona ya kwamba watu wangu wanachukuliwa bure

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Ninaona adui akichukua watu wangu bure"

bure

Maana zaweza kuwa 1) "bure" ina maana Wababeli walichukua watu bila haki na bila sababu au 2) hii inaendelea sitiari kutoka 52:2 ambapo Yahwe anazungumziwa kana kwamba alimiliki watu wa Israeli na anaweza kuwatoa bure.

Wale wanaotawala juu yao wanadhihaki

Hii ina maana ya Wababeli ambao wamewashinda watu. Hata hivyo, baadhi ya tafsiri zina, "Wale ambao hutawala juu yao wanalia". Kwa tafsiri hizi, kipande hiki kina maana ya viongozi wa Waisraeli walio katika kifungo.

jina langu linakashifiwa mfululizo siku nzima

Hapa "jina" inawakilisha sifa ya Yahwe. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "wale ambao hutazama aduii akichukua watu wangu wanaendelea kusema mambo mabaya juu yangu"

Kwa hiyo watu wangu watalijua jina langu

Hapa "jina" inawakilisha sifa ya Yahwe. "Kwa hiyo watu wangu watanijua mimi ni nani kiukweli"

Isaiah 52:7

Maelezo ya Jumla

Isaya anazungumza na watu wa Israeli

Jinsi iliivyo mizuri juu ya milima ni miguu ya wajumbe wanaoleta habari njema

Hapa "miguu" inawakilisha mjumbe ambaye anatembea. "Ni vizuri kuona mjumbe akija juu ya milima kutangaza habari njema"

kwa Sayuni

Hapa "Sayuni" inawakilisha watu wa Sayuni. "kwa watu wa Sayuni"

paza sauti zao

Hii ni lahaja. "paza sauti"

kila jicho lao

Hapa "macho" yanawakilisha mtu mzima. "kila mmoja wao"

Isaiah 52:9

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

enyi uharibifu wa Yerusalemu

Isaya anazungumzia uharibifu wa Yerusalemu kana kwamba ulikuwa mtu ambaye angeweza kushangilia. Hii inawakilisha watu wa Yerusalemu ambao walishindwa. "nyie watu ambao mnaishi miongoni mwa uharibifu wa Yerusalemu"

amemkomboa Yerusalemu

Hapa "Yerusalemu" inawakilisha watu. "amewakomboa watu wa Yerusalemu"

amafunua mkono wake mtakatifu

Hapa "mkono" inawakilisha nguvu ya Yahwe. Yahwe kuonyesha watu wote wa mataifa ya kwamba ni mtakatifu na mwenye nguvu inazungumziwa kana kwamba Yahwe alikuwa shujaa aliyetoa joho lake, kufunua mikono yake kwa ajili ya vita. "alionyesha utakatifu wake na nguvu yake kuu"

mataifa yote; dunia yote

Hapa "mataifa" na "dunia" inawakilisha watu wa mataifa yote katika dunia yote.

Isaiah 52:11

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Ondoka, ondoka

Neno hili linarudiwa kusisitiza ya kwamba watu wanapaswa kuondoka haswa, ingawa sio mara hiyo hiyo.

Ondoka kutoka hapa

Inachukuliwa kuwa watu wa Israeli walikuwa watumwa wa Babeli. Hii naweza kuwekwa wazi. "ondoka kutoka katika nchi ambapo ni mtumwa"

usiguse chochote kichafu

Kitu ambacho Yahwe amesema hakifai kuguswa au kuliwa inazungumziwa kana kwamba kilikuwa kichafu kimwili. "usiguse kitu ambacho hakikubaliki kwa Yahwe"

ondoka miongoni mwake

Hapa "mwake" inawakilisha Babelii

Yahwe atakwenda mbele yako; na Mungu wa Israeli atakuwa mlinzi wako wa nyuma

Yahwe kulinda watu wake kutoka kwa maadui inazungumziwa kana kwamba alikuwa hodari ambao huondoka mbele ya watu na hodari wanaobakii nyuma ya watu kuwalinda.

Isaiah 52:13

atakuwa juu na kuinuliwa, na atainuliwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. Misemo hii miwili "juu na kiinuliwa juu" na "atainuliwa" ina maana moja na inasisitiza ya kwamba Yahwe ataheshimu mtumishi wake. "Nitampa mtumishi wangu heshima kubwa"

walivyokuogopa wewe

Hapa "wewe" ina maana ya mtumishi wa Yahwe. Hata hivyo, watafsiri wanaweza kubadili "wewe" kuwa "yeye".

muonekano wake uliharibiwa sana kuliko ule wa mtu yeyote

Inachukuliwa ya kwamba mtumishi anaharibiwa kwa sababu adui walimpiga sana. Maana kamili inaweza kuwekwa wazi. "adui zake hupiga mwili wake vibaya sana hadi hakuonekana kama binadamu tena"

Isaiah 52:15

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza juu ya mtumishii wake.

mtumishi wangu atanyunyizia mataifa mengi

Mtumishi kusababisha watu wa mataifa kukubaliika kwa Yahwe inazungumziwa kana kwamba mtumishi alikuwa kuhani anayenyunyizia damu ya sadaka kufanya mtu au kitu kukubalika kwa Yahwe.

atanyunyizia

Neno la Kiebrania lilitafsiriwa "kunyunyizia" hapa linaweza kutafsiriwa kama "mshangao" au "shtusha", ambavyo baadhi ya tafsiri za Biblia hufanya.

mataifa mengi

Hapa "mataifa" yanawakilisha watu wa mataifa.

wafalme watafunga midomo yao

Msemo "kufunga midomo yao" ni lahaja. "wafalme wataacha kuzungumza" au "wafalme watakaa kimya"

kile ambacho hawakuambiwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "kile ambacho hakuna mtu alichowaambia" au "kitu ambacho hakuna mtu alichowaambia"

Isaiah 53

Isaiah 53:1

Maelezo ya Jumla

Hapa Isaya anafafanua matukio ambayo yatatokea katika siku za usoni kana kwamba yametokea kipindi cha nyuma. Hii inasisitiza ya kwamba yatatokea hakika.

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kufafanua mtumishi wa Yahwe.

Ni nani aliyeamini kile walichosikia kutoka kwetu

Kile ambacho Yahwe amegundua ni ajabu sana hadi anashangaa kama walio uhamishoni wataamini. "walichosikia" inajumlisha yeye na wale walio uhamishoni. "Ni vigumu kw yeyote kuamini kile alichosikia"

na ni kwa nani mkono wa Yahwe umefunuliwa?

Mkono una maana ya nguvu ya Yahwe. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "na Yahwe amefunua nguvu yake kwa watu"

Kwa maana alikua mbele ya Yahwe kama mti mchanga

Hapa "alikua" ina maana ya mtumishi wa Yahwe ambaye Isaya anamlinganisha na mti mchanga sana. Hii inasisitiza ya kwamba ataonekana dhaifu.

kutoka katika nchi iliyokauka

"nchi iliyokauka" ni ardhi ngumu na iliyokauka ambayo hairuhusu mimea kuota na inawakilisha wapi mtumishi wa Yahwe atakuja. "kutoka katika hali isiyowezekanika"

Isaiah 53:3

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kufafanua mtumishi wa Yahwe.

Alidharauliwa na kukataliwa na watu

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Watu walimchukulia kuwa si kitu na kumkataa"

mtu mwenye huzuni

"mwanamume ajuaye kila aina ya huzuni"

kwa watu ambao huficha nyuso zao

"Uso" inawakilisha dhamira ya mtu au jumuiya. Kuficha uso wa mtu kugeuka kutoka kwa mtu. "kwa watu ambao wanageuka"

alidharauliwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "walimchukulia kutokuwa na thamani"

Isaiah 53:4

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kumfafanu mtumishi wa Yahwe.

amechukua ugonjwa wetu na kubeba huzuni zetu

"Kuchukua" au kubeba usahaulifu kama ugonjwa na huzuni inawakilisha kuuchukua. "amechukua ugonjwa wetu na huzuni juu yake mwenyewe"

ingawa tulidhani ya kuwa aliadhibiwa na Mungu, alipigwa na Mungu, na kuteswa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "ingawa tulidhani Mungu alikuwa akimuadhibu na kumtesa"

Isaiah 53:5

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kumfafanua mtumishi wa Yahwe.

Lakini alitobolewa kwa sababu ya matendo yetu ya uasi; alipondwa kwa sababu ya dhambi zetu

Misemo hii miwili ina maana moja na inasisitiza ya kwamba mtumishi aliteseka kwa sababu ya dhambi za watu. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Mungu aliwaruhusu maadui kumchoma na kumua kwa sababu ya dhambi zetu"

Adhabu kwa ajili ya amani yetu ilikuwa juu yake

Hii ina maana ya amana na Mungu. Hii inaweza kuwekwa wazi. "Alipokea adhabu hii ili tuweze kuishi katika upatanifu"

kwa majeraha yake tunaponywa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "alituponya kwa mateso ya majeraha yake"

Isaiah 53:6

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kumfafanua mtumishi wa Yahwe.

Sisi wote kama kondoo wamepotoka

Kondoo mara kw mara huacha njia ambayo mchungaji huwaongoza. Isaya ana maana ya kwamba tunafanya kile tunachotaka badala ya kile Mungu anavyoamuru.

udhalimu wetu wote

"Udhalimu" hapa unawakilisha hatia kwa ajili ya dhambi yetu. "hatia kwa ajili ya dhambi ya kila mmoja wetu"

Isaiah 53:7

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kumfafanua mtumishi wa Yahwe.

Alikandamizwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Walimtendea kwa ukatili"

hakufungua kinywa chake

"Kinywa" inawakilisha kile ambacho mtu husema. Kufungua kinywa cha mtu ina maana ya kuongea. "hakupinga"

kama mbuzi ambaye huongozwa machinjioni, na kama kondoo aliye mbele ya wakata manyoya alivyo mtulivu

Isaya analinganisha mtumishi kwa mbuzi na kondoo kusisitiza ya kwamba atabaki kimya wakati watu wakimdhuru na kumuaibisha.

kama mbuzii ambaye huongozwa machinjioni

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "kama mbuz alivyo kimya mtu anapomchinja"

Isaiah 53:8

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kumfafanua mtumishi wa Yahwe.

Kwa kuonewa na kuhumiwa alishutumiwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Walimtendea kwa ukatili, wakamhukumu, na wakamshutumu"

kuonewa

Neno la Kiebrania linatafsiriiwa hapa kama "kuonewa" na baadhi ya tafsiri kama "kukamata". Kwa tafsiri hizi, wazo ni kuwa Mtumishii atakamatwa na kisha kuhukumiwa na kushutumiwa.

nani kutoka kizazi hicho alimfikiria tena juu yake?

Swali hili linasisitiza ya kwamba hakuna mtu anayemfikiria. "hakuna mtu kutoka kizazii chake aliyejali nini kilitokea kwake" au "hakuna mtu kati ya walioishi naye walijali nini kilitokea kwake"

nani kutoka kizazi hicho alimfikiria tena juu yake?

Tafsiri nyingi zinatafsiri sehemu hii kwa Kiebrania tofauti. "Nani anaweza kusema jambo juu ya uzao wake? au "Nani anaweza kusema kitu kuhusu hatma yake?"

lakini aliondolewa kutoka katika nchi ya walio hai

"Kuondolewa" hapa ina maana ya kifo. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Lakini alikufa" au "Lakini kifo kikamchukua"

ya watu wangu

"ya watu wa Israeli"

wala hapakuwa na udanganyifu katika kinywa chake

"Kinywa" inawakilisha kile mtu anachosema. "wala hakumdanganya yeyote alipozungumza"

Isaiah 53:10

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kumfafanua mtumishi wa Yahwe.

ataona uzao wake

Hapa "uzao" una maana ya wale watu ambao Yahwe amewasamehe kwa sababu ya sadaka ya mtumishi.

atarefusha maisha yake

Hii inazungumzia kumfanya aishi kwa muda zaidi. "Yahwe atamfanya mtumishi wake kuishi tena"

kusudi la Yahwe litatimizwa kupitia kwake

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe atatimiza kusudi lake kupitia mtumishi wake"

Baada ya mateso ya maisha yake

Hapa "maisha yake" ina maana ya mtumishi. "Baada ya mtumishi kuteseka"

ataona nuru

tafsiri nyingi zinaelewa "nuru" hapa kumaanisha uhai. Yaani, mtumishi atakuwa hai tena.

Mtumishi wangu mtakatifu

Hapa "wangu" ina maana ya Yahwe

atabeba udhalimu wao

"kubeba" hapa ina maana ya kubeba na inawakilisha mtumishi wa Yahwe kuchukua hatia ya dhambi yao. "atachukua hatia yao juu yake mwenyewe"

Isaiah 53:12

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kumfafanua mtumishi wake.

Kwa hiyo nitampatia sehemu yake miongoni mwa makundi, na atagawanya marupurupu na wengi

Vishazi hivi viwili vina maana moja. "Sehemu" na "marupurupu" ina maana ya mfalme baada ya ushindi vitani kugawanya vitu vilivyotekwa nyara au zawafi na jeshi lake. Hii ina maana Mungu atamheshimu sana mtumishi wake kwa sababu ya sadaka yake.

makundi

Tafsiri nyingi inatafsiri msemo huu kama "wengi" au "wenye nguvu"

kwa sababu alijiweka wazi kwa kifo

"Kujiweka wazi" ina maana ya kuwa wazi au hatarishi. Mtumishi wa Yahwe alijiweka katika hali ambayo angeweza kufa. "alikubali kwa hiari uwezekano wa kifo"

na alihesabiwa na wavunja sheria

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "na kuruhusu watu kumtendea kama mhalifu"

Isaiah 54

Isaiah 54:1

wewe mwanamke tasa ... watoto wa mwanamke aliyeolewa

Yahwe kuwaambia watu wa Yerusalemu kufurahi kwa sababu kutakuwa na watu wengi wakiishi katika Yerusalemu tena inazungumziwa kana kwamba Yahwe alikuwa akimwambia mwanamke tasa atakwenda kuwa na watoto wengi.

imba kwa shangwe ya furaha na kulia kwa sauti, wewe ambaye hujawahi kuwa katika uchungu

Kauli hii ina maana moja na sehemu ya kwanza ya sentensi.

Kwa maana watoto wa mwenye ukiwa ni zaidi

Tukio ambalo litatokea katiika siku za usoni linazungumziwa kana kwamba limetokea kipindi cha nyuma. Hi inasisitiza ya kwamba tukio hakika litatokea. "Kwa maana watoto wa mwanamke mwenye ukiwa atakuwa zaidi"

mwenye ukiwa

Hapa "mwenye ukiwa" ina maana mume wa mwanamke alimkataa na kumuacha.

Isaiah 54:2

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Yerusalemu.

Fanya hema lako kubwa ... imarisha vigingi vyako

Hii inaendeleza sitiari ambayo ilianza katika 54:1. Yahwe kuwaambia watu wa Yerusalemu kuandaa kwa sababu Yahwe ataongeza watu wake inazungumziwa kana kwamba anamwambia mwanamke kufanya hema lake kubwa kutengeneza chumba kwa ajili ya watoto wengi.

Kwa maana utasambaa

Hapa "utatawanyika" ni umoja na ina maana ya mwanamke tasa. Anawakilisha vizazi vyake vyote. "Kwa maana wewe na vizazi vyako mtasambaa kote"

vitatawala mataifa

Hapa "mataifa" yanawakilisha watu. "watawashinda watu w mataifa mengine"

Isaiah 54:4

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Yerusalemu.

utasahau aibu ya ujana wako na fedheha ya kutelekezwa kwako

Yahwe kuwaambia watu ambao wapo katika siku za usoni kuwa hata hawatafikiri juu ya aibu waliyopitia pale adui zao walipowashinda inazungumziwa kana kwmba Yahwe alikuwa akimwambia mwanamke ya kwamba hatafikiri tena juu ya aibu aliyopitia kwa kutoweza kupata watoto na mume wake kumtelekeza.

Isaiah 54:5

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Yerusalemu.

Kwa maana Muumba wako ni mume wako

Yahwe kuwapenda na kuwatunza watu wake inazungumziwa kana kwamba alikuwa mume wao.

Muumba

Muumba wa watu.

Yahwe wa majeshi

Yahwe wa majeshi ya Israeli.

Mtakatifu wa Israeli

Mtakatifu wa Israeli

Mkombozi

Mkombozi wa Israeli

anaitwa Mungu wa ulimwengu wote

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "yeye ni Mungu wa dunia nzima"

Yahwe amekuita tena kama mke ... kama mwanamke aliyeolewa kijana na kukataliwa

Yahwe kuwatuma watu wake katika uhamisho na kisha kuwarudisha inazungumziwa kana kwamba Yahwe alikuwa mume ambaye alimkataa mke wake lakini sasa anampokea.

na kuhuzunika rohoni

Hapa "roho" inawakilisha kiumbe cha ndani cha mtu. "na kuhuzunishwa" au "na kuwa na huzuni"

Isaiah 54:7

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Yerusalemu.

Katika hasira iliyofurika

Yahwe kuwa na hasira sana inazungumziwa kana kwamba hasira yake ilikuwa mafuriko ambayo yanawazidi watu. "Nilipokuwa na hasira sana"

Nimeficha uso wangu kutoka kwako

Hapa "kuficha uso wangu" ni lahaja ambayo ina maana ya Mungu kutelekeza watu wake na kuwaacha wateseke. "Nilikutelekeza"

lakini kwa agano la uaminifu la milele

Nomino dhahania "uaminifu" inaweza kuwekwa kama "mwaminifu". "lakini kwa sababu mimi ni mwaminifu siku zote kwa agano langu na wewe" au "lakinii kwa sababu mimi ni mwaminifu kufanya kile nilichoahidi kufanya"

anasema Yahwe, ambaye anakuokoa wewe

Hapa Yahwe anazungumzia juu yake katiika mtu wa tatu. Inaweza kuwekwa katika mtu wa kwanza. "hivi ndivyo mimi, Yahwe, mkombozi wako, nasema kwako"

Isaiah 54:9

maji ya Nuhu

Hii ina mana ya mafuriko ambayo Yahwe alisababisha wakati wa kipindi cha Nuhu.

Ingawa milima inaweza kuanguka na vilima kutikiswa, bado upendo wangu wa kudumu

Yahwe anafafanua hali ya kubuni kufafanua kile kitakachotokea hata kama masharti yalifiikiwa. "Hata kama milima ilianguka na vilima kutetemeka, upendo wangu wa kudumu"

vilima kutikiswa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "vilima vinaweza kutikisika"

upendo wangu wa kudumu hautageuka kutoka kwako

Yahwe kuendelea kuwapenda watu wake inazungumziwa kana kwamba upendo wake hautaweza kugeuka kutoka kwa watu. "sitaacha kukupenda"

wala agano langu la amani kutikiswa

Yahwe kutofutilia agano lake na watu inazungumziwa kana kwamba agano lake lilikuwa chombo ambacho kinaweza kutikisika. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "na sitafuta agano langu la amani" au "na kwa hakika nitakupa amani kama nilivyoahidi katika agano langu"

anasema Yahwe, ambaye ana rehema juu yako

Hapa Yahwe anazungumza juu yake katika utatu. Inaweza kuwekwa katika mtu wa kwanza. "hivyo ndivyo mimi, Yahwe, nayetenda kwa rehema, nasema"

Isaiah 54:11

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Yerusalemu.

Aliyeteswa

Hapa Yahwe anazungumzia mji wa Yerusalemu kana kwamba ulikuwa ukimsikiliza. Hapa Yerusalemu inawakilisha watu ambao wanaishi pale. "nyie watu mlioteswa wa Yerusalemu"

aliyeendeshwa kwa dhoruba

kuendeshwa Yahwe anazungumzia watu kana kwamba walipulizwa na kuharibiwa kwa upepo na dhoruba. Hii ina maana ya watu kuumizwa na kukosa uthabiti.

asiyefarijika

"bila faraja"

Nitatengeneza njia yako ya miguu katika rangi ya feruzi ... ukuta wa mawe mazuri

Yahwe anafafanua katika maneno ya kiufundi jinsi atakavyorejesha Yerusalemu na kusababisha iwe nzuri tena. Ingawa lugha inaweza kukuzwa.

feruzi ... johari... rubi

Hivi ni vito vya thamani. Feruzi ni rangi ya bluu ya kijani, johari na bluu iliyoiva, na rubi ni rangi nyekundu iliyopauka.

Isaiah 54:13

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Yerusalemu.

Kisha watoto wako wote watafundishwa na Yahwe

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Na Yahwe atawafundisha watoto wako wote"

na Yahwe

Yahwe anajizungumzia mwenyewe katika utatu. Inaweza kuwekwa katika mtu wa kwanza. "kwa mimi, Yahwe"

Katika haki nitakuimarisha tena

Nomino dhahania "haki" inaweza kuwekwa kama kivumishi "sahihi". "Nitasababisha uwe na nguvu tena kw sababu utafanya kile kilicho sahihi"

na hakuna kitu cha kutisha kitakuja karibu nawe

Hii ina maana hakuna mtu katika mji au walio nje wataweza kuwatisha wakazii wa Yerusalemu tena

Isaiah 54:15

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Yerusalemu.

anachokonoa matatizo

Hii ni lahaja. "inasababisha taabu" au "inakutaabisha"

ataanguka katika kushindwa

Hii ni lahaja. "utawashinda katika vita"

Isaiah 54:17

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Yerusalemu.

Hakuna silaha ambayo inaundwa dhidi yako itafanikiwa

Maadui kutofanikiwa dhidi ya watu wa Yahwe inazungumziwa kana kwamba silaha zao hazitaweza kufanikiwa dhidi ya watu wa Yahwe. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Maadui wanweza kutengeneza silaha kukushambulia lakini hawatakushinda"

Huu ni urithi wa watumishi wa Yahwe

Dhawabu ambayo Yahwe atawapa wale ambao watamtumikia inazungumziwa kana kwamba dhawabu ilikuwa kitu watakachoweza kurithi.

hili ni tamko la Yahwe

Yahwe anajizungumzia katika utatu. Hii inaweza kuwekwa katika mtu wa kwanza. "hivi ndivyo mimi, Yahwe, navyotamka"

Isaiah 55

Isaiah 55:1

Kauli Kiunganishi

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Yerusalemu katika uhamisho kupitia Isaya.

Taarifa ya Jumla

Yahwe anazungumzia kubariki watu kwa uhuru kana kwamba alikuwa akiuza chakula na vinywaji kwa watu wahitaji bure.

Njooni ... njooni

Marudio ya neno hili mara nne linaongeza wazo la uharaka wa mwaliko.

nunua divai na maziwa bila pesa na bila gharama

Kuna fasili ya dhana akilini ya kejeli katika kauli hii kwa maana mtu kawaida anapaswa kutumia pesa kununua kitu. Hii inasisitiza neema ya ajabu ya Yahwe katika kutoa vitu hivi bure.

Isaiah 55:2

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Yerusalemu.

Kwa nini unapima uzito wa fedha kwa kile kisicho mkate?

Yahwe anauliza swali hili kukaripia watu. Anazungumza juu ya watu kutafuta furaha kando na Yahwe kana kwamba walikuwa wakinunua vitu kula ambavyo havikuwa chakula. "Haupaswi kupima fedha kwa kile ambacho ni mkate"

unapima uzito wa fedha

Hii ina maana ya kuhesabu sarafu za fedha ili kumlipa mtu kwa ajili ya kitu. "lipa pesa"

kwa kile kisicho mkate

Hapa neno "mkate" unawakilisha chakula kwa ujumla. Inadokezwa ya kwamba watu walikuwa wakinunua vitu kula ambavyo havikuwa chakula halisi. "kwa vitu vya kula ambavyo sio chakula halisi"

kwa nini unafanya kazi kwa kile hakiridhishi?

Yahwe anauliza swali hili kukaripia watu. Anawazungumzia kutafuta furaha tofauti na kwa Yahwe kana kwamba walikuwa wakifanya kazi kupata pesa kununua vitu ambavyo haviwezi kuwaridhisha. "haupaswi kufanya kazi kwa ajili ya pesa kutumia kwa vitu ambavyo haviridhishi"

kula kilicho chema, na ufurahie katika unene

Watu kumtumaini Yahwe kwa kumbariki na furaha inazungumziwa kana kwamba wanakula chakula kizuri ambacho kinawafanya wawe na furaha.

katika unene

Neno "unene" lina maana ya nyama ambayo ina mafuta mengi juu yake na ni lahaja kwa chakula kizuri. "kwa vyakula vizuri"

Isaiah 55:3

Geuza masikio yako

Kusikiliza au kuzingatia kwa makini juu ya mtu inazungumziwa kana kwamba ilikuwa kugeuza masikio ya mtu kwa mtu.

upendo mwaminifu ulioahidiwa kwa Daudi

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "upendo mwaminifu ambayo nimemuahidi Daudi"

Nimemuweka

Maana zaweza kuwa 1) hii ina maana ya kile Yahwe alifanya kwa Mfalme Daudi kipindi cha nyuma au 2) ina maana ya kile ambacho Mungu atafanya kupitia mmoja wa vizazi vya Daudi.

Isaiah 55:5

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza kwa watu wa Yerusalemu.

Mtakatifu wa Israeli

Mtakatifu wa Israeli, yaani Yahwe

Isaiah 55:6

Mtafute Yahwe wakati bado anaweza kupatikana

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Mtafute Yahwe wakati bado unaweza kumpata"

Na muovu aache njia yake

Neno "muovu" una maana ya watu waovu. Yahwe anazungumzia watu waovu kutofanya dhambi tena kana kwamba walikuwa wakiacha kutembea katika njia ambayo walikuwa wakisafiria. "Na watu waovu wabadili namna wanavyoishi"

na mwanamume wa dhambi mawazo yake

Kitenzi unaweza kutumika kutoka katika msemo uliopita. "na mwanamume mwenye dhambi aache mawazo yake"

mawazo yake

Maana zaweza kuwa 1) "namna anavyofikiri" au 2) "mipango yake"

naye atamhurumia

"na Yahwe atamhurumia"

na kwa Mungu wetu

Kitenzi kinaweza kutumika kutoka kwa msemo wa kwanza katika sentensi hii. "na mruhusu arudi kwa Mungu wetu"

Isaiah 55:8

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Yerusalemu.

hili ni tamko la Yahwe

Hii inaweza kutamkwa tofauti ili kwamba nomino dhahania "tamko" linawekwa kama kitenzi "tamkwa" au "kusema kwa dhati". "hiki ndicho Yahwe alichotamka" au "hiki ndicho Yahwe alichosema kwa dhati"

kama vile mbingu zilivyo juu kuliko dunia, kwa hiyo ndivyo njia zangu zilivyo juu kuliko njia zako, na mawazo yangu kuliko mawazo yako

Yahwe anazungumzia mambo anayofanya na jinsi anavyofikiri kama kuwa bora zaidi au juu zaidi kuliko watu wanavyofanya au kufikiri, kama jinsi mbingu ilivyo juu sana kuliko nchi.

Isaiah 55:10

Taarifa ya jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Yerusalemu.

Kama vile mvua na theluji ... havirudi kule

Hii inawezekana ni ufafanuzi wa mvua na theluji kuvukiza.

kwa hiyo pia neno langu ... litafanikiwa kwa kile ambacho nimekituma

Yahwe anazungumza juu ya neno lake kana kwamba lilikuwa mtu ambaye anamtuma kama mjumbe wake kuhitimisha kazi.

neno langu litakuwa ambalo linatoka kinywani mwangu

Hapa neno "mdomo" unawakilisha Yahwe mwenyewe. "neno ambalo nazungumza"

halitarudi kwangu bila manufaa

Hapa ufafanuzi wa neno kurudi kwa Yahwe lina maana ya kwamba imemaliza kazi ambayo Yahwe ameituma kukamilisha. Ya kwamba haitarudi "bila manufaa" ina maana ya kwamba haitashindwa kutimiza kazi yake. "Haitashindwa kukamilisha kazi yake"

lakini itatimiza kile ambacho ninachotaka, na itafanikisha kile nilichokituma

Misemo hii miwili kimsingi ina maana moja na inasisitiza ya kwamba kile Yahwe anasema kitaendelea kufanyika. "lakini nitatimiza kile nachotaka, na mambo nayozungumza nitasababisha yafanyike"

Isaiah 55:12

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Yerusalemu.

kuongozwa mbele kwa amani

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Nitakuongoza mbele kwa amani"

milima na vilima itabomoka kwa kelele za shangwe mbele yako, na miti yote ya shambani itapiga makofi

Yahwe anazungumzia milima, vilima na miti kana kwamba vilikuwa watu na sauti na mikono, vikisherehekea pale Yahwe anapowaokoa watu wake.

Badala ya miba ya vichaka, mvinje utaota; na badala ya mtemba, mti wa mihadasi utaota

Maneno "miba ya vichaka" na "mvinje" ina maana ya aina ya mimea ambayo ina miba mikali inayoota juu yao. Maneno "mvinje" na "mtemba" una maana ya aina ya miti ya kijani. Mimea ya miba inaashiria ukiwa, wakati ukijani unaashiria uzima na mafanikio.

kwa jina lake

Hapa neno "jina" linawakilisha umaarufu wa Yahwe. "kwa umaarufu wake" au "kwa heshima yake"

ambayo haitakatwa mbali

Kitu kinachokoma kuwepo kinazungumziwa kana kwamba kinakatwa mbali, kama tawi linavyokatwa mbali na mti au kipande cha kitambaa kinavyokatwa kutoka kwenye nguo. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "ambalo halitafika mwisho" au "ambalo itadumu milele"

Isaiah 56

Isaiah 56:1

kwa maana wokovu wangu upo karibu, na haki yangu inakaribia kufunuliwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Hivi punde nitakuokoa na kukuonyesha ya kwamba nina haki"

ambaye anaishikilia kwa nguvu

Hapa "anaishikilia kwa nguvu" ni lahaja ambayo ina maana ya kuendelea kuchunguza kitu. "ambaye ni mwangalifu kuendelea kufanya hivi"

kuzuia mkono wake kufanya uovu wowote

Hapa "mkono" ina maana ya matendo ya mtu au tabia. "hafanyi mambo maovu"

Isaiah 56:3

Tazama, mimi ni mti mkavu

Hii ina maana matowashi walifikiri wangeweza kuwa sehemu ya watu wa Mungu kwa sababu walibadilishwa kwa kuhanithishwa (na kwa sababu hii hawawezi kupata watoto). Waisraeli hawafanya zoezi la kuhasi, wageni walifanya, mara nyingine kama adhabu. Matowashi ambao walipokea imani ya waebrania walijua ya kwamba kawaida hawakuruhusiwa kuabudu katika hekalu (Kumb. 23.1). Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi.

Isaiah 56:4

katika nyumba yangu na katika kuta zangu

Misemo hii miwili ina maana moja. "ndani ya kuta za hekalu langu"

ambayo hatakataliwa mbali

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ambayo haitaisha" au"ambayo haitasahaulika"

Isaiah 56:6

wanaojiunga kwa Yahwe

Hii ina maana ya wageni ambao wamejiunga na watu wa Yahwe.

wanaolipenda jina la Yahwe

"jina" linawakilisha tabia na utu wa Yahwe. "wanaompenda Yahwe"

mlima mtakatifu

"Mlima mtakatifu" ni Mlima Sayuni, katika Yerusalemu. "katika mlima mtakatifu wote wa Yahwe"

zitapokelewa juu ya madhabahu yangu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Nitapokea juu ya madhabahu yangu"

nyumba yangu itaitwa nyumba ya maombi

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "nyumba yangu itakuwa nyumba ya maombi"

Isaiah 56:9

Nyie wote wanyama wa mwitu wa shambani, njooni na mmeze, nyie wanyama wote wa msituni

Mungu aliwaita majeshi wa mataifa mengine kwa kuwalinganisha na wanyama kuja na kushambulia watu wa Israeli.

Walinzi wao wote ni vipofu

Hii ina maana ya viongozi wa Israeli hawawezi au labda hawataki kuona kile kinachotendeka katika jamii.

Wote ni mbwa walionyamaza

Viongozi wanatakiwa kufungua vinywa vyao na kuwaonya watu, lakini hawafanyi hivyo. Kulinganisha mtu na mbwa katika jamii hii ni fedheha kubwa.

Wanaota, na kujilaza chini wanapenda kulala

Hii ina maana viongozi hawaleti neno la Mungu la kuwaonya Waisraeli lakini wanapenda zaidi starehe yao.

Isaiah 56:11

Muhtasari wa Jumla

Yahwe anaendelea kufafanua viongozi waovu wa watu wake.

Mbwa wana hamu kubwa ya kula

Yahwe anaendelea kulinganisha viongozi wabaya wa Israeli na mbwa.

Isaiah 57

Isaiah 57:1

watu wa agano la uaminifu

"watu ambao wana haki na kushika sheria ya Mungu" au "watu ambao ni waaminifu kwa Mungu"

wanakusanywa mbali ... wanapumzika katika vitanda vyao

Zote hizi zina maana ya kufa.

ya kwamba mwenye haki anakusanywa mbali kutoka katika uovu

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "ya kwamba watu wenye haki hufa, na Yahwe huwachukua mbali kutoka kwa chote kilicho kiovu"

Anainga katika amani

"Wenye haki huingia katika amani"

wale wanaotembea katika unyofu

"wale ambao wamefanya kilicho sahihi"

Isaiah 57:3

Lakini njooni hapa

Mungu anawaita watu wote ambao sio waaminifu kuja mbele yake ili awahukumu katika utofauti mkubwa kwa ahadi kwa ajili ya wenye haki waliotangulia.

wana wa mwanamke mchawi

Hii ni fedheha kubwa dhidi ya watu ambao hufanya uchawi kwa sababu uchawi na mazingombwe hujumuisha kuabudu sanamu.

watoto wa mzinzi na mwanamke ambaye amejifanya kuwa kahaba

Hii ina maana ya uzinzi halisia na wa kiroho. Wamemuacha kuabudu Mungu na sasa wanaabudu miungu mingine pamoja na ukahaba halisia katika sherehe za Wakaanani.

Ni nani ambaye unafurahia kumdhihaki? Ni dhidi ya nani unafungua mdomo na kuchomoza ulimi wako?

Yahwe anatumia maswali kukaripia watu ambao wanamdhihaki kupitia kuabudu kwa uongo. "Mnanidhihaki na kunikejeli kwa kufungua mdomo wako wazi na kuchomoza nje ulimi!"

Je! wewe siye watoto wa uasi, watoto wa udanganyifu?

Yahwe anatumia swali lingine kukaripia watu. Hii haimanshi kuzaliwa kwao lakini hali yao ya kiroho. "Nyie ni watoto wa uasi, watoto waa udanganyifu!"

Isaiah 57:5

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wasio waaminifu wa Israeli.

Mnajipatia joto wenyewe ... chini ya mawe yalitokeza

Matendo haya yote yanahusishwa na kuabudu sanamu. Mialoni ilikuwa miti mitakatifu kwa Wakaanani. Watu walidhani matendo haya yangeongeza rutuba kwa watu na kwa nchi.

Isaiah 57:6

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza kwa watu wasio waaminifu wa Israeli.

ambavyo vimegawiwa kwako

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. Maana hasa katika iiebrania haipo wazi. "hilo ni fungu lako" au "huo ni urithi wako"

Je! nifurahi katika hivi vitu ?

Yahwe anatumia swali kukaripia watu. "Hakika, vitu hivi havinifurahishi"

Isaiah 57:7

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza kwa watu wasio waaminifu wa Israeli.

Uliandaa kitanda chako

Hii ina maana ya kulala na kahaba kama sehemu ya kuabudu miungu ya uongo.

juu ya mlima wa juu

Watu mara kwa mara walienda juu ya vilima na milima kuabudu miungu ya uongo. Walidhani hizo zilikuwa sehemu bora za kuabudu. Hii inaweza kumaanisha Yerusalemu, pia.

Ulifanya agano pamoja nao

"Ulifanya mkataba na mimi"

Isaiah 57:9

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza kwa watu wasio waaminifu wa Israeli.

ulishuka chini Kuzimu

Watu hawakwenda kuzimu kihalisia, dunia ya wafu. Badala yake, Yahwe anaonyesha ya kwamba watu walikuwa tayari kwenda popote kutafuta miungu wapya wa kuabudu.

Ulipata maisha mikononi mwako

Baada ya kujaribu sana, waabudu sanamu waligundua kuwa bado wana nguvu ya kuendelea. Hapa "mkono" una maana ya "nguvu" au "uwezo"

Isaiah 57:11

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza kwa watu wasio waaminifu wa Israeli.

Ni nani uliye na wasiwasi juu yake? Ni nani unayemuogopa sana ambaye amasababisha kutenda kwa udanganyifu ... juu yangu?

Yahwe anatumia maswali haya kukaripia watu. "Inaonekana unaogopa kabisa sanamu hizi kwako utende kwa udanganyfu ... juu yangu!"

sana mpaka huwezi kunikumbuka au kufikiria juu yangu

Misemo hii miwili ina maana moja na inasisitiza ya kwamba, ingawa watu walitakiwa kumkumbuka Yahwe, hawakufanya hivyo.

Nitatangaza matendo yako yote ya haki na kusema yote ambayo umeyafanya

Yahwe anawakejeli, kwa kuita matendo yao ya uovu haki.

Isaiah 57:13

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza kwa watu wasio waaminifu wa Israeli.

acha kusanyiko lako la sanamu likuokoe

Yahwe anawadhihaki watu na sanamu zao. Anaziambia sanamu kuwaokoa watu ingawa anajua haziwezi.

upepo utaubeba wote mbali, pumzi itazibeba zote mbali

Hii ni kusema jambo moja kwa njia mbili kusisitiza ya kwamba sanamu hazijiwezi na hazina thamani. "upepo, hata pumzi, itazipuliza mbali"

mlima mtakatifu

"Mlima matakatifu" ni Mlima Sayuni, katika Yerusalemu.

Isaiah 57:14

Jenga, jenga! Safisha njia! Ondoa vitu vyote vya kujikwaa kutoka katika nja ya watu wangu

Yahwe ana nguvu na haraka ya kwamba njia ya wazi na tambarare iweze kuwepo kwa watu kurudi kwake na kufungulia vikwazo kwa kumuabudu Yahwe. Hii inaitikia 40:3.

Kwa maana hiki ndicho Yule aliye juu na kuinuliwa asemavyo

Maneno "juu" na "kuinuliwa" kimsingi ina maana moja hapa na inasisitiza Yahwe kuinuliwa.

kufufua roho ya wanyenyekevu, na kufufua moyo ya wenye majuto makali

Misemo hii miwili ina maana moja na inasisitiza ya kwamba Yahwe atawatia nguvu na kutia moyo wale ambao wanajishusha mbele yake.

roho ... moyo

Hapa hizi zina maana ya mawazo ya mtu na hisia, sio roho na moyo kihalisia.

Isaiah 57:16

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Nimeficha uso wangu

Hii ina maana ya Mungu alikata tamaa kwa watu wake na hakuwasaidia au kuwabariki.

alikwenda kwa nyuma katika njia ya moyo wake

Hii ina maana ya Waisraeli waliendelea kumkataa Mungu wa kwelii kwa wa uongo. Hapa "nyuma" na "njia" ni maneno ya mahali yanayowakilisha motisha na hisia.

Isaiah 57:18

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza.

njia zake

"njia zao". Hapa "zake" ina maana ya watu wa Israeli.

fariji na tuliza wale ambao wanaomboleza kwa ajili yake

"Nitabembeleza na kutuliza wale ambao wanahisi huzuni kwa ajili ya mateso ya watu kwa sababu ya tabia yao ya dhambi"

na ninatengeneza matunda ya midomo

Hapa "matunda ya midomo" ina maana ya kile mtu anachosema. "na ninasababisha wao wanisifu na kunishukuru"

Amani, amani, kwa wale ambao wapo mbali sana

"Nimefanya amani pamoja nao ambao wako mbali" Neno "Amani" linarudiwa kwa msisitizo.

Isaiah 57:20

Lakini waovu ni kama bahari inayorusharusha ... takataka na matope

Hii inalinganisha waovu na maji yenye vurugu katika ufuko yanayofanya maji kuwa machafu.

Isaiah 58

Isaiah 58:1

Inua sauti yako kama tarumbeta

Hii ina maana kupiga kelele kwa sauti. Hapa "yako" ina maana ya Isaya.

Wakabili watu wangu kwa uasi wao, na nyumba ya Yakobo kwa dhambi zao

Misemo hii miwili ina maana moja. Kwa pamoja wanaimarisha uharaka kukabili watu wa Yahwe.

Isaiah 58:3

'Kwa nini tumefunga', wanasema, 'lakini hauioni? Kwa nini tumejishusha, lakini hautambui?'

Watu wa Israeli wanatumia maswali kulalamika kwa Mungu kwa sababu wanahisi hawajali.

Isaiah 58:4

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kwa kujibu swali lao la changamoto.

Tazama

"Tazama" or "Zingatia kwa makini". Yahwe anawakabili swali lao kwa kuwaambia kuzingatia kwa makini.

ngumi ya uovu

"ngumi ya uovu". Hii inaonyesha wanapigana kwa ukali. "Ngumi" inawakilisha hasira ambayo ni vurugu ya mwili.

Je! hii ni aina ya kufunga ambayo ningetaka ... chini yake?

Yahwe anatumia swali kukaripia watu. Wanajifanya kana kwamba ni wanyenyekevu mbele ya Mungu, lakini wanawaumiza watu wengine. "Hii sio aina ya kufunga ninayoitaka ... chini yake"

Siku kwa ajili ya mtu yeyote kujishusha, kwake kuinamisha chini kichwa chake kama matete

Hii ina maana mtu anainama chini, lakini sio mnyenyekevu ki ukweli. "Tete" linawakiliisha mmea dhaifu ambao hujikunja kirahisi.

Je! unata hivi kufunga kweli, siku ambayo inampendeza Yahwe?

Yahwe anatumia swali kukaripia watu. "Hakika haufikiri aina hii ya kufunga inanifurahisha!"

Isaiah 58:6

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Isareli.

Je! hii sio kufunga ambayo naichagua ...kuvunja kila nira?

Yahwe anatumia swali kufundisha watu kuhusu aina ya kufunga ambayo inamfurahisha. "Hii ni kufunga ninayochagua ... kuvunja kila nira".

Kufungua vifungo vya waovu, kufungua kamba za nira, kuwaweka waliokanyagwa huru, na kuvunja kila nira

Misemo hii yote ina maana ya kwamba wanatakiw kuwasaidia watu wle ambao waovu na wanawaumiza na kuwakandamiza.

Je! sio ku ... nyumba yako?

Yahwe anatumia swali lingine kuwafundisha watu. "Ni ku... nyumba yako".

vunja mkate wako

Msemo huu unawakilisha kuanza mlo kwa mwenyeji kuchana mkate.

Isaiah 58:8

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Kisha nuru yako itavunjwa wazi kama mapanzuko

"Vunja wazi" ni lahaja ambayo ina maana ya pale ambapo nuru huanza kuwaka kwa mwanga. Hii ina maana ya kwamba kama watawasaidia watu wahitaji, matendo yao yatakuwa kama nuru inayoonwa na wengine, kama jua linavyochomoza baada ya giza la usiku. Au mwanga unaweza kumaanisha nuru ya Bwana, inayowaka juu yao na kuwabariki.

na uponyaji wako utachipuka juu kwa haraka

Hii ina maana Mungu atawabariki na kuwarudisha haraka, kama kidonda kinavyopona haraka.

haki yako itakuwa mbele yako, na utukufu wa Yahwe utakuwa ulinzi wako wa nyuma

Hii ina maana ya kipindi ambapo Mungu aliwalinda watu wa Israeli walipotoroka kutoka Misri. Hii ina Mungu atawalinda tena kutoka kwa adui zao watakapofanya kilicho sahihi.

haki yako

Msemo huu katika Kiebrania unaweza kutafsiriwa kama yule anayetoa haki au hata ushindi. Katika muktadha huu, msemo huu ungemaanisha Mungu. Tafsiri za kisasa zina tafsiri hii.

Isaiah 58:9

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

kisha nuru yako itainuka kutoka gizani, na giza lako litakuwa kama mchana

"Nuru yako" inawakilisha matendo ya wema ambayo yatakuwa mifano kwa kila mtu, na "giza" ni matendo mabaya, yatashindwa kwa matendo yao mema.

Isaiah 58:11

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli

kukuridhisha katika maeneo ambapo hakuna maji

"Maji" inawakilisha kila kitu wanachohitaji kwa ajili ya maisha tele hata kama mazingira yake hayana ya kutosha.

utakuwa kama bustani iliyomwagiliwa

"Bustani iliyomwagiliwa" inawakilisha wingi ili waweze kuwa na yote wanayohitaji.

kama chemchemi ya maji, ambayo maji yake hayakosi

"Chemchemi ya maji" inawakilisha chanzo cha wingi katika nchi ambapo maji ni ya thamani.

Isaiah 58:12

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli

utaitwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "watu watakuita"

Isaiah 58:13

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli

unageuza miguu yako kutoka na kusafiri katika siku ya Sabato, na kutofanya starehe yako katika siku yangu takatifu

Hapa "miguu" ina maana ya safari na kazi ambayo wtu walifanya katika siku zingine zote. Mungu hakuruhusu safari ndefu au kazi katika siku ya kupumzika. "unaacha kusafiri na kufanya unachotaka kufanya katika siku ya Sabato, siku yangu takatifu"

Isaiah 58:14

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Nitakufanya uendeshe katika vilele vya dunia

Hii ina maana ya Mungu kunua taifa katika sifa na nguvu kwa mwitikio wa kuishi katika haki.

kwa maana kinywa cha Yahwe kimenena

"kinywa" inaashiria kile ambacho Yahwe anasema. "Kwa maana Yahwe amekisema"

Isaiah 59

Isaiah 59:1

Tazama

"Tazama!" "Unapaswa kujua!" Yahwe anawaambia watu kuzangatia kwa makini.

Mkono wa Yahwe sio mfupi sana

"Mkono" unawakilisha nguvu na uwezo. "Mkono mfupi hauna nguvu na uwezo. "Yahwe anaweza kabisa"

yako ...yamekutenga

Viwakilishi hivi vya wingi vina maana ya watu wa Israeli kama kundi moja.

dhambi zako zimemfanya afiche uso wake kwako

"Uso" unawakilisha kuwepo sasa na kutazama juu ya. "dhambi zako zimekufanya ugeuke kutoka kwako"

Isaiah 59:3

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Kwa maana mikono yako imetiwa doa kwa damu na vidole vyako kwa dhambi

Hapa "mikono" na "vidole" ina maana ya matendo yao. Hii ina maana wana hatia ya kufanya mambo makali na ya dhambi. "vyako" ni wingi. "Kwa maana umetenda dhambi kali"

Midomo yako inazungumza uongo na ulimi wako unazungumza kwa nia mbaya

Sehemu za mwili ambazo hutoa maneno na kuwakilisha kile watu wanasema. "Unazungumza uongo na mambo maovu"

wanatunga mimba ya taabu na kuzaa dhambi

"Kupata mimba" na "kuzaa" inasisiitiza jinsi wanavyopanga kwa makini kufanya mambo ya dhambi. Hapa "wanatunga" bado ina maana ya watu wa Israeli. "wanafanya kazi kwa bidii kufanya mambo ya dhambi"

Isaiah 59:5

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli kuhusu maovu wanayofanya kwa kutumia sitiari ya nyoka wenye sumu na wavu za buibui.

Wanatotoa mayai ya nyoka wenye sumu

Mayai ya nyoka wenye sumu kutotoa kuwa nyoka hatari zaidi. "Nyoka wenye sumu" inawakilisha uovu ambao watu hufanya ambao unadhuru zaidi na zaidi. "Wanafanya uovu ambao husambaa kutengeneza uovu zaidi"

kufuma wavu wa buibui

Hii inawakilisha matendo ya watu ambayo hayana thamani. "wanazaa vitu na matendo ambayo hayana thamani"

Yeyote anayekula mayai yao hufa, na iwapo yai likipondwa, linatotoa kuwa nyoka wa sumu

Kula yai lenye sumu litamuua mtu ambaye analila na inawakilisha kujiangamiza. Kuvunja yai huruhusu nyoka wadogo wenye sum kutotoa na inawakilisha kusambaa kwa uharibifu. "Matendo wanayofanya yatawaangamiza na kusambaza uharibifu kwa wengine"

iwapo yai likipondwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "kama mtu akiponda yai"

Nyavu zao haziwezi kutumiwa kwa ajili ya mavazi, wala hawawezi kujifunika kwa kazi zao

Hii ina maana matendo yao maovu hayawezi kufunikwa na kufichwa, kama vile wavu hauwezi kufanya nguo na kumfunika mtu. "Matendo yao maovu yatafunuliwa kuwa bila thamani"

Nyavu zao haziwezi kutumiwa kwa ajili ya mavazi

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Hawawezi kuvaa nguo kwa wavu zao"

Matendo ya vurugu yamo mikononi mwao

"mikono" inawakilisha uwezo na nguvu ya kufanya vitu hivi na kwa hiyo jukumu lao. "wana wajinu kamili kwa vurugu wanayofanya"

Isaiah 59:7

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kzungumza na watu wa Israeli.

Miguu yao hukimbilia uovu

"Miguu" inawakilisha uwezo wa kuondoka na "kukimbia" ina maana ya kufanya jambo kwa haraka. "Wana haraka ya kufanya mambo maovu"

ni njia zao

"njia" inawakilisha njia yao ya maisha. "ni yote wanayofanya"

hakuna haki katika njia zao

"njia" inawakilisha njia yao ya maisha. "kamwe hawafanyi kilicho haki" au "kila kitu wafanyacho sio cha haki"

Wametengeneza njia zilizopinda

"Njia zilizopinda" inawakilisha njia ya maisha ambayo imepotoka. "Wanasema na kufanya mambo yasiyo ya kweli. Ni wajanjawajanja"

Isaiah 59:9

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

haki ipo mbali kutoka kwetu

Hapa "kwetu" ina maana ya Isaya na watu wa Israeli. "Mbali" inawakilisha haki iliyotoweka na ngumu kupata. "haki imetoweka na ngumu sana kupata"

Tunasubiri kwa ajili ya nuru, lakini tunaona giza; tunatafuta mwanga, lakini tunatembea gizani

Kila ya hii misemo ina maana ya kwamba watu wanasubiri wema wa Mungu, lakini inaonekana kana kwamba amewatelekeza.

Tunapapasa ukuta kama vipofu ... kama watu waliokufa

Hii ina maana ya kwamba kwa sababu Mungu haji kwao, wanajisikia bila msaada, kutopata njia sahihi na kukata tamaa na siku za usoni, bila tumaina la maisha ya kusisimua.

Isaiah 59:11

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Tunaunguruma kama dubu na kunung'unika kama njiwa

Hii ina maana ya sauti ambayo watu walifanya kwa sababu walikuwa na dhiki na maombolezo.

Isaiah 59:12

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza.

makosa yetu mengi

Hapa "yetu" ina maana ya Isaya na watu wa Israeli.

mbele zako

Hapa "yako" ina maana ya Yahwe.

dhambi zetu zinashuhudia dhidi yetu

Isaya anafafanua dhambi kama mtu anavyokwenda mbele za Mungu kutamka ya kwamba watu wana hatia.

kwa maana makosa yetu yapo pamoja nasi

"pamoja nasi" inawakilisha kutambua uwepo wao. "kwa maana tunatambua makosa yetu"

Isaiah 59:14

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza.

Haki imerudishwa nyuma

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Watu wanasukuma haki nyuma"

Haki ... haki ... kweli ... uadilifu ... Uaminifu

Haya ni mawazo ambayo Isaya anafafanua kama kujifanya kama watu

Isaiah 59:16

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza.

Aliona ya kwamba hakuna mtu, na akashangaa ya kwamba hapakuwa na mtu wa kuingilia kati.

"Yahwe alishtushwa ya kwamba hakuna mtu alikua kuwasaidia wale waliokuwa wakiteseka" au "Yahwe alishangazwa ya kwamba hakuna mtu aliyekuja kuwasaidia wale waliokuwa wakiteseka"

Kwa hiyo mkono wake mwenyewe ulileta wokovu kwa ajili yake

"'mkono" unawakilisha uwezo na nguvu. "Yahwe alitumia nguvu yake mwenyewe kuwaokoa watu"

na haki yake ikamsaidia

"Haki" ni sifa ambayo hujifanya kama mtu. "na alifanya sahihi kama anavyofanya siku zote"

Isaiah 59:17

Akavaa haki kama dereya ya kifuani na kofia ya chuma ya wokovu juu ya kichwa chake. Alijivisha mavazi ya kisasi na kuvaa ari kama joho

"dereya", "kofia ya chuma", "mavazi", na "joho" ni nguo kwa ajili ya vita na kupigana, Isaya anamfafanua Yahwe kama akivaa haya kuwaadhibu watu wake.

joho

joho lililo huru, linalotiririka

Akawarudishia maliipo

Isaya anafafanua tukio la siku za usoni kana kwamba ilitokea kipindi cha nyuma. Hii ina maana hakika itatokea.

Isaiah 59:19

Maelezo ya Jumla

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "'ambayo pumzi ya Yahwe huongoza"

wataogopa jina la Yahwe

Hapa "jina" lina maana ya sifa ya Yahwe na tabia. "muogope Yahwe"

kutoka magharibi ... kutoka kwa mawio ya jua

Isaya anaunganisha maneno haya mawili kumaanisha watu katika maeneo yote duniani.

kwa maana atakuja kama kijito kinachokuja kwa kasi

Mabonde membamba ya Yuda yalikuwa yamekauka muda mwingi katika mwaka hadi pale mvua nzito ya ghafla ilipogeuza kuwa maji yanayokwenda kwa kasi. Hicho kilipotokea kulikuwa na kelele nyingi na upepo.

kinachoendeshwa kwa pumzi ya Yahwe

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "ambayo pumzi ya Yahwe inaendesha"

tamko la Yahwe

Hii inaweza kuandikwa ili kwamba nomino dhahania "tamko" liwe kitenzi "alitamka" au "alisema kwa dhati". "Hivi ndivyo Yahwe alivyotamka" au "Hiki ndicho Yahwe alichosema kwa dhati"

Isaiah 59:21

maneno yangu ambayo nimeweka kinywani mwako

Hii ina maana ya kumpatia mtu kitu cha kusema. "ujumbe niliokpatia kuzungumza"

Isaiah 60

Isaiah 60:1

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Inuka, angaza; kwa maana nuru yako imekuja, na utukufu wa Yahwe umeinuka juu yako

Hii ina maana ya vtu vitukufu Yahwe amevifanya kwa wakazi wa Yerusalemu. Zipo kwa ajili ya kuonyesha utukufu huo kupitia kile vinavyofanya na kusema na kuwa na tumaini katika siku za usoni.

Isaiah 60:2

Maelezo ya Jumla

Isaya anazungumza na watu wa Israeli. Anaendelea sitiari ju ya "mwanga"

Ingawa giza litafunika dunia, na giza nene mataifa

Misemo hii miwili ina maana moja na inajumlishwa kwa msisitizo. Ina maana ya "giza la kiroho". Hii ina maana watu wengine wote wa dunia hawatamjua Yahwe au namna ya kumpendeza. Hii ni sitiari kwa hukumu takatifu.

bado Yahwe atainuka juu yako

Hii ina maana mwanga wa uwepo wa Mungu utatokea kwa ajili ya watu wa Israeli, na utaonekana njia wanayopaswa kwenda.

na utukufu wake utaonekana juu yako

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "na watu wa mataifa wataona utukufu wake juu yako"

Isaiah 60:4

Maelezo ya Jumla

Hapa Yahwe anaanza kuzungumza.

Wote wanajikusanya

"Wote" ina maana ya watu waliobakii wa Israeli ambao watakuja pamoja kurudi Yerusalemu.

binti zako watabebwa mikononi mwao

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "watabeba binti zako mikononi mwao" au "watabeba binti zako juu ya viuno vyao"

Kisha utatazama na kung'aa, na moyo wako utashangilia na kumwagikia

Misemo hii inatumia maana moja na kusisitiza ya kwamba watakuwa na furaha sana kwa sababu ya kile kitakachotokea Yerusalemu.

wingi wa bahari

Hii ina maana ya utajiri na bidhaa ambazo zitakuja Yerusalemu kwa njia ya meli, labda kupitia Bahari ya Mediteranea.

utamwagwa nje kwako

Hii inaelezea ya kwamba wingi utakuwa kama maji ambayo yanabubujika nje.

Isaiah 60:6

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

ngamia

"ngamia wadogo"

Efa ... Kedari ... Nebayothi

Haya ni majina ya maeneo ya Uarabuni.

Makundi yote ya Kedari yatakusanywa pamoja kwako

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Watu wa Kedari watakusanya makundi yao kwa ajilii yako"

kondoo wa Nebayothi watatumikia mahitaji yako

Hii ina maana ya hitaji lao la kutoa sadaka.

watakuwa sadaka inayokubalika juu ya madhabahu yangu

Mimi, Yahwe, nitazipokea juu ya madhabahu yangu"

Isaiah 60:8

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Hawa ni kina nani wanaopaa kama wingu, na kama njiwa katika makazi yao?

Yahwe anatumia maswali na picha za kishairi kuvuta nadhari hapa. Analinganisha matanga ya meli kwa mawingu na njiwa. Hii pia ni taswira ya Waisraeli kurudi katika nchi ambapo wanaishi. "Tazama, ninaona kitu kama mawingu yakisogea haraka na kama njiwa wakirudi katika makazi yao"

Pwani

Hii ina maana ya watu ambao wanaishi katika pwani na inafafanua eneo la pwani kana kwamba ilikuwa watu wakiangalia nje. "Watu kutoka pwani"

meli za Tarshishi

Msemo huu kawaida una maana ya meli kubwa za biashara zinazofaa kwa safari ndefu.

Mtakatifu wa Israeli

Mtakatifu wa Israeli

amekuheshimu

"Yahwe amekuheshimu, watu wa Israeli"

Isaiah 60:10

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

hayatafungwa mchana na usiku

Hapa "mchana" na "usiku" pamoja ina maana ya "wakati wote". Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "hakuna atakayeweza kuvifunga"

ili kwamba utajiri wa mataifa uweze kuletwa, na wafalme wake wakiwa wameongozwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "ili kwamba watu wa mataifa waweze kuleta utajiri wao, pamoja na wafalme wao"

Isaiah 60:12

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

mataifa hayo yataangamizwa kabisa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Nitaangamiza kabisa watu wa mataifa hayo"

utukufu wa Lebanoni

Hii ina maana ya Lebanoni kuwa maarufu kwa miti yake mizuri, haswa mvinje na seda. Utambuzi hasa wa miti yote haujulikani.

sehemu ya miguu yangu

Hii ina maana ya hekalu la Yahwe.

Isaiah 60:14

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Mtakatifu wa Israeli

Mtakatifu wa Israeli

Isaiah 60:15

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

bila mtu yeyote anayepi katikati yako

"na kila mtu akiepuka nchi yako" au "na kila mgeni akiepuka nchi yako"

Pia utakunywa maziwa ya mataifa, na utanyonya katika ziwa la wafalme

Hii ina maana ya utajiri na wing ambao utanyonywa kutoka kwa mataifa ya kigeni. Vishazi vyote vinarudia wazo moja kwa msisitizo.

Mkombozi

Mkombozi wa Israeli.

Mwenye enzi wa Yakobo

Mwenye enzi wa Israeli

Isaiah 60:17

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

badala ya mbao, shaba, na badala ya mawe, chuma

Yahwe atatoa vifaa vya thamani zaidi vya ujenzi kwao sasa. "badala ya mbao, nitaleta shaba, na badala ya mawe, nitaleta chuma"

Nitateua amani kama mkuu wako, na haki watawala wako

Yahwe anafafanua "amani" na "haki" kama watawala wa kibinadamu. Hii ina maana kutakuwa na amani kamili na haki katika nchi ya Israeli.

Vurugu haitasikika tena katika nchi yako

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Hakutakuwa tena na taarifa za vurugu katika nchi yako"

lakini utaita kuta zako Wokovu, na malango yako Sifa

Viumbo vya kihalisia vina majina ya sifa za kiroho. Mji wa Yerusalemu utakuwa eneo salama, na watu pale watamsifu Yahwe.

Isaiah 60:19

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

kwa maana Yahwe atakuwa nuru yako ya mlele

Mistari miwili inarudia wazo hili moja kwa msisitizo.

Jua lako halitazama tena, wala mwezi wako hautaondoka na kupotea

Mwezi hautapotelea kihalisia. Hii ni kusema ya kwamba kulinganisha na mwanga wa Yahwe, mwanga wa jua na mwezi hautakuwa kitu.

Isaiah 60:21

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

tawi la kupanda kwangu, kazi ya mikono yangu

Misemo hii ina maana karibu moja na inarudiwa kwa ajili ya msisitizo.

tawi la kupanda kwangu

Yahwe analinganisha watu kwa mmea mchanga kuota ambao alipanda kana kwamba alikuwa mkulima wa bustani. Yahwe ameweka watu wake katika nchi ya Israeli. Hii inatoa matumaini kwa watu.

kazi ya mikono yangu

Yahwe analinganisha watu wa Israeli kwa kitu kilichoundwa kwa ujuzi wa mkono wake.

ili kwamba niweze kutukuzwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "ili kwamba watu wote waweze kunitukuza"

elfu moja

"1,000"

Isaiah 61

Isaiah 61:1

Roho wa Bwana Yahwe yupo juu yangu

"Roho" hapa ni Roho Mtakatifu wa Yahwe ambaye humsukuma au kuhamasisha mtu.

walioteswa

Hii ina maana ya watu maskiniu, wale walio ndani ya huzuni kubwa, au watu walioteswa ambao wana matatizo wanaoshindwa kuyatatua wao wenyewe.

uhuru kwa wafungwa, na kufungua kwa gerez kwa wale waliofungwa

Misemo hii miwili ina maana moja. Inasema ya kwamba Mungu kwa hakika atatoa uhuru kwa wafungwa.

Isaiah 61:2

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza

mwaka wa fadhila ya Yahwe, siku ya kisasi

Misemo hii miwili ina maana ya muda mmoja wa wakati. "Mwaka" na "siku" zote ni mifano bayana ambayo inawakilisha ukubwa kamili.

mwaka wa fadhila ya Yahwe

"wakati ambapo Yahwe atatenda wema kwa watu wake"

Isaiah 61:3

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza.

kuwapa ... kuwapatia

Isaya anarudia hivi kusisitiza.

kilemba

"kilemba cha kichwani" au "kifuniko kizuri cha kinywani". Hii ni kitambaa kirefu cha nguo kinachozunguka kichwa.

mafuta ya furaha ... joho la sifa

Watu huweka mafuta juu yao na kuvaa joho zuri, ndefu wakati wa sherehe na shangwe.

katika nafasi ya roho ya kutojali

"katika nafasi ya huzuni" au "katika nafasi ya maombolezo"

mwaloni wa utakatifu, kupandwa kwa Yahwe

Hii ina maana Yahwe amesababisha watu kuwa na nguvu na imara.

ili aweze kutukuzwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "ili kwamba maisha ya watu yaweze kumtukuza yeye"

Isaiah 61:4

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza kutumia usambamba katika kila mstari.

Isaiah 61:6

Taarifa ya Jumla

Mtumishi wa Yahwe anaendelea kuzungumza kwa watu wa Israeli na kila mstari kuwa sambamba.

Utaitwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Watu watakuita"

utapata mara mbili

Huenda hii ina maana ya fungu mara mbili la nchi.

watafurahi juu ya mgawo wao ... wata ... nchi yao ... itakuwa yao

Hii bado ina maana ya watu wa Israeli. Hii inaweza kuwekwa katika hali ya mtu wa pili. "utafurahia juu ya gawio lako ... uta ... nchi yako ... itakuwa yako"

Isaiah 61:8

Vizazi vyao vitajulikana miongoni mwa mataifa, na watoto wao miongoni mwa watu

Vishazi hivi viwili vina maana moja. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Watu kutoka mataifa mengine watajua vizazi vyao"

watoto wao miongoni mwa watu

Kishazi hiki kinachukulia kitenzi hicho hicho kama kilicho nyuma. "uzao wao utajulikana miongoniu mwa watu"

Isaiah 61:10

Nitafurahi sana katika Yahwe

"Nita" ina maana ya watu wa Mungu wakizungumza kama mtu mmoja ambaye Yahwe amerejesha.

amenivisha kwa mavazi ya wokovu; amenivisha na joho la utakatifu

Watu wa Mungu kuzungumza kama mtu mmoja sasa wa wokovu na utakatifu kama muonekano wao tofauti unavyoonekana kwa wote. "Mavazi" na "joho" ni nguo ambazo kila mtu anaweza kuona.

kama bwana arusi anavyojipamba na kilemba, na kama bibi arusi anavyojiremba na vito vyake

Mlinganisho huu unasisitiza ya kwamba mwandishi ana furaha sana, anasherehekea.

kilemba

"kilemba cha kichwani" au "kifuniko kizuri cha kinywani". Hii ni kitambaa kirefu cha nguo kinachozunguka kichwa.

Kwa maana kama nchi izaavyo mimea yake inayochipuka, na kama bustani inavyofanya mimea yake kuota

Huku ni kusema kitu kima kwa njia mbili. Ukweli ya kwamba chochote Mungu anachosema atafanya hakika kitafanyika kinalinganishwa na ukweli kwamba mbegu huchipuka baada ya kupandwa. "Kama vile mbegu zinavyopandwa katika bustani huchipuka kutoka kwenye udongo na kuota"

utakatifu na sifa kuchipuka juu

Msemo huu unaelezea sifa hizi kama kuota kutoka kwa mbegu kama mimea inavyofanya.

Isaiah 62

Isaiah 62:1

Kwa ajili ya Sayuni sitanyamaza, na kwa ajili ya Yerusalemu sitakaa kimya

Kauli hizi mbili zina maana moja. Hapa "Sayuni" na "Yerusalemu" zote zinawakilisha watu wanaoishi katika Yerusalemu. "Kwa ajili ya watu wa Yerusalemu sitanyamaza"

sitakaa kimya

Inawezekana ya kwamba "sitakaa" ina maana ya Isaya

mpaka utakatifu wake utakapojitokeza

Vishazi hivi viwili vinaaminisha watu wa Mungu hatimaye kurudi na kuokoa watu wa Israeli na kwamba itakuwa dhahiri kama mwanga ulivyo.

Isaiah 62:3

Pia utakuwa taji la uzuri mikononi mwa Yahwe, na kilemba cha kifalme mkononi mwa Mungu wako

Hizi zina maana moja na zinaunganishwa kwa ajili ya msisitizo. Zinasema ya kwamba Yerusalemu utakuwa mji wa kifalme chini ya nguvu na mamlaka ("mkono") ya Mungu.

haitakuwa kwako tena ... kusemwa, "Ukiwa"

Hizi zina maana moja na zinaunganishwa kwa ajili ya msisitizo.

haitasemwa kwako tena

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Watu hawatasema tena juu yako"

wala nchi yako haitasemwa tena

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "wala watu hawatasema tena juu ya nchi yako"

na nchi yako itaolewa

Hii ina maana Yahwe atawapenda watu wa Israeli na atakuwa nao daima kama alivyo mume.

Isaiah 62:5

kama vile mwanamume anavyomuoa mwanamke, vivyo hivyo wana wako watakuoa

Hapa "wana" ina maana ya watu wa Israeli na "wako" ina maana ya Yuda, nchi ya Israeli. Hii ina maana ya kwamba watu watamiliki nchi kama vile mwanamume anavyomiliki mke wake kijana.

kama vile bwana arusi anavyofurahia bibi arusi wake, Mungu wako atafurahi juu yako

Hii inasisitiza furaha ya Mungu juu ya uhusiano wake na watu wake.

Isaiah 62:6

Nimeweka

Hapa "Nimeweka" inaweza kumaanisha Isaya au Yahwe.

walinzi katika kuta zako

Hii ina maana ya manabii, maafisa, au yawezekana malaika, ambao wanaomba kila wakati kwa ajili y watu wa Yerusalemu kama walinzi ambao hulinda mji kila wakati.

hawako kimya mchana na usiku

Hii ina maana wanamsihi Yahwe kwa muendelezo au kujia wao kwa wao. "wanaomba kwa dhati kwa Yahwe katika siku nzima"

Usimruhusu apumzike

Hapa "apumzike" ina maana ya Yahwe.

Isaiah 62:8

kwa mkono wake wa kuume na kwa mkono wa nguvu yake

Mkono wa kuume unawakilisha nguvu na mamlaka. "kwa nguvu na mamlaka yake"

Hakika sitakupatia tena mazao kama chakula kwa ajili ya adui zako

Hii ina maana Yahwe hatawaruhusu adui zake kuwashinda watu wa IUsraeli na kuchukua mazao yao tena. Huenda maadui walichukua mazao kipindi cha nyuma kama ushuru au kulisha majeshi yao wenyewe.

Sitakupatia tena mazao kama chakula kwa ajili ya adui zako ... Wageni hawatakunywa divai yako mpya

Kauli hizi zimewekwa pamoja kwa ajili ya msisitizo au ukamilifu.

wale watakaovuna mazao ... wale wanaochuma mizabibu

Kauli hizi zinawekwa pamoja kwa ajili ya msisitizo na ukamilifu.

Isaiah 62:10

Njoo upite, njoo upite katika malango

Msemo "njoo upite" unarudiwa kuonyesha uharaka.

Ijenge, Ijenge njia

Neno "jenga" linarudiwa kusisitiza ya kwamba Yahwe anataka kwa uharaka barabara kuandaliwa. "Njia" inawakilisha njia ambayo watu watarudi. Hii ni sawa na 40:3 na 57:14.

Kusanya mawe

"Chukua mawe kutoka barabarani kuifanya iwe laini. Mawe yanawakilisha vipingamizi vyote vya safari kuwa haraka.

Nyanyua ishara ya bendera kwa ajili ya mataifa

Bendera ya ishara inawakilisha kitu kuvuta nadhari ya wengine. Hii ina maana Yahwe anawaita watu wa mataifa mengine kugundua nchi ya Israeli na kuona kile Yahwe alichofanikisha kama alivyosema angefanya.

Isaiah 62:11

Tazama

"Gundua"

mwisho wa dunia

Sehemu za dunia ambazo zipo mbali sana zinazungumziwa kana kwamba zilikuwa sehemu ambapo nchi hufikia kikomo. Msemo huu pia unaunda neno moja kwa kundi la mambo mengi na lina maana ya kila sehemu kati ya miupaka. "sehemu za mbali za dunia" au "dunia nzima"

binti Sayuni

"Binti" inawakilisha watu wa Yerusalemu (Sayuni).

Tazama, dhawabu yake ipo pamoja naye, na fidia yake inakwenda mbele yake

Vishazi hivi vinawakilisha wazo moja kwa msisitizo.

utaitwa

Hii inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda, "watakuita"

Isaiah 63

Isaiah 63:1

Ni nani huyu ajaye kutoka Edomu ... Bosra

Isaya anazungumza kama mlinzi kwa kutumia mfumo wa swali na jibu kuwakilisha taarifa hii juu ya hukumu ya Yahwe kwa Edomu, adui wa Israeli. Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Mimi, Yahwe, ninakuja kutoka Edomu, nikiwa nimevaa mavazi mekundu kutoka Bosra"

Bosra

Huu ni mji mkuu wa Edomu.

Ni Mimi

Hapa "Mimi" ina maana ya Yahwe.

Kwa nini nguo zako ni nyekundu, na kwa nini ... kishinikizo cha zabibu

Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Wekundu katika nguo zako zinakufanya uonekane kana kwamba ulikuwa ukikanyaga ju ya zabibu katika kishinikizo cha zabibu"

kishinikizo cha zabibu

Kishinikizo cha zabibu ni sehemu ya chini iliyochongwa kwa jiwe katika ardhi ambapo wafanyakazi hukanyaga zabibu kuziponda kwa miguu yao, ili kutoa juisi ya zabibu.

Isaiah 63:3

Nina zabibu zilizokanyagwa

Hapa "Nina" ina maana ya Yahwe. Picha hii ina maana ya Yahwe kuangamiza adui zake.

Kwa maana ninatazamia siku ya kisasi

Hapa "siku" ina ya kipindi cha muda.

kisasi

Yahwe ataadhibu kwa njia sahihi kuleta haki. Aina yake ya ukombozi inatofautiana na kisasi cha mtu.

mwaka wa ukombozi

Hapa "mwaka" ina maana ya muda bayana uliowekwa na Yahwe kurejesha Israeli.

Isaiah 63:5

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza

lakini mkono wangu wenyewe

Hapa "mkono" unawakilisha uwezo.

na kuwafanya walewe katika hasira yangu

Hii ina maana Yahwe aliwafanya washangae na kutokuwa na ufahamu wa hasira yake kamili na adhabu.

nilimwaga nje damu yao

Hapa "damu" inawakilisha maisha ya adui wa Yahwe ambao walikuw wakimwagika nje ili waweze kufa.

Isaiah 63:7

Nitasema

Hapa "Nitasema" ina maana ya Isaya

alichotufanyia kwetu

Hapa "kwetu" ina maana ya Isaya na watu wa Israeli.

Isaiah 63:9

Katika mateso yao yote

"Katika mateso yao yote". Hapa "yao" ina maana ya watu wa Israeli. Isaya anajumuisha yeye kama mwanajumuiya wa watu.

aliteseka pia

Hapa "aliteseka" ina maana ya Yahwe.

malaika kutoka katika uwepo wake

Hii inawakilisha nani aliyetumwa kutoka katika uwepo wa Mungu.

aliwainua juu na kuwabeba

Hii ina maana ya pale Mungu aliwalinda na kuwaokoa watu wa Israeli kutoka kwa Wamisri miaka mingi mapema. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi.

Isaiah 63:10

Lakini waliasi

"lakini tuliasi". Hapa "waliasi" ina maana ya watu wa Israeli. Isaya anajijumlisha kama mwanajumuiya wa watu.

Roho wake Mtakatifu

"Roho Mtakatifu wa Yahwe"

Isaiah 63:11

Walisema

"tulisema". Hapa "walisema" ina maana ya watu wa Israeli. Isaya anajijumlisha kama mwanajumuiya wa watu.

ambaye aliwatoa kutoka katika baharii

Simulizi ya Yahwe kugawanya maji ya Bahari ya Matete kimiujiza ili kwamba Waisraeli waweze kuvuka na kuwatoroka Wamisri ni taarifa inayosadikiwa.

wchungaji wa kundi lake

Viongozi mara nyingine wanajulikana kama "wachungaji". "viongozi wa watu wake"

Isaiah 63:12

Maelezo ya Jumla

Watu wa Israeli wanaendelea kuzungumza.

ambaye altengeneza nguvu yake tukufu iende pamoja na mkono wa kuume wa Musa

Hapa "mkono wa kuume" inawakilisha nguvu ya Yahwe kupitia Musa. Hii ina maana ilikuwa nguvu ya Mungu ambayo ilimwezesha Musa kugawanya maji katika Bahari ya Matete.

Kama farasi akimbavyoo katika nchi tambarare, hawakujikwaa

Hii ina maana ya kwamba watu wa Israeli walikuwa na miguu ya hakika kama ya farasi katika nchi ya wazi katika safari zao kuelekea Israeli kutoka Misri.

Isaiah 63:14

Maelezo ya Jumla

Watu wa Israeli wnaendelea kuzungumza.

Kama mifugo inavyokwenda chini katika bonde ... pumziko

Picha hii inaonyesha mifugo kushuka katika bonde ambapo kuna nyasi za kijani na maji na inasisitiza ya kwamba Mungu aliwaongoza watu wa Israelii na kuwatunza.

kujifanyia mwenyewe jina la sifa

Hapa "jina la sifa" ina maana ya heshima na sifa ya mtu. "hakikisha una sifa ya kuheshimiwa kwa ajili yako"

Isaiah 63:15

Maelezo ya Jumla

Watu wa Israeli wanaendelea kuzungumza.

Iko wapi ari yako na matendo yako makuu?

Mwandishi anatumia swali kuonyesha hisia za ndani na kujali kwa sababu inaonekaba Mungu hawasaidii. Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Hatuoni ari yako na matendo yako makuu!"

Huruma yako na matendo yako ya upole yamewekwa kutoka kwetu

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Unaficha huruma yako na upole kutoka kwetu"

ingawa Abrahamu hatujui, na Israeli hatutambui

Mababu hawa wa taifa la Israeli wasingeweza kutambua vizazi vyao kwa sababu walibadilika sana. "Abrahamu" na "Israeli" wanawakilisha wakati wa zamani.

Isaiah 63:17

Maelezo ya Jumla

Watu wa Israeli wanaendelea kuzungumza.

Yahwe, kwa nini unatufanya tuzurure kutoka katika njia zako na kuifanya mioyo yetu kuwa migumu, ili kwamba tusikutii wewe?

Hapa mwandishi anatumia swali kuelezea lalamiko la watu wa Mungu. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Yahwe umetufanya tuzurure kutoka katika njia zako na kuwa wakaidi ili kwamba tusikutii"

kwa nini unatufanya tuzurure kutoka katika njia zako

Kutofanya kile ambacho Yahwe anaamuru inazungumziwa kana kwamba mtu anazurura kutoka katika njia sahihi. "kwa nini unatufanya kufanya kilicho kibaya"

kuifanya mioyo yetu kuwa migumu

Hii ina maana kutoweza kukataa mafundisho ya Yahwe kwa kukataa kusikiliza na kutii. Hapa "moyo" unawakilisha nia, hisia na shauku zao.

Isaiah 63:18

Maelezo ya Jumla

Watu wa Israeli wanaendelea kuzungumza.

ambao hawakuitwa kwa jina lako

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "jina" ina maana ya uhusiano wa familia. "ambaye hakuwa mmoja wa familia yako"

Tumekuwa ... hawakuitwa kwa jina lako

Baadhi ya tafsiri za kisasa zinatafsirii sehemu hii tofauti. "Tumekuwa kama watu ambao haujawatawala, kama wale ambao hawajaitwa kwa jina lako"

Isaiah 64

Isaiah 64:1

Taarifa ya Jumla

Watu wa Israeli wanaendelea kuzungumza kwa Yahwe.

O! kama unge

Isaya anatambulisha haja hii kwa uwepo wa Yahwe katika kipindi cha nyuma kwa mshangao mkubwa.

kama ungepasua wazi mbingu

Kama Yahwe amejionyesha kwa mbwembwe kwa kupasua wazi mbingu. Maneno "kupasua wazi" yana maana ya kuchana kipande cha nguo mbalimbali.

milima ingetetemeka

Milima ingeweza kutetemeka kama vile tetemeko.

kama pale moto uwashao misitumisitu, au moto unaofanya maji kuchemka

Hii yawezekana kusisitiza jinsi uwepo wa Mungu ungeweza kusababisha kwa urahisi milima na watu kutetemeka.

Isaiah 64:3

Taarifa ya Jumla

Watu wa Israeli wanaendelea kuzungumza na Yahwe.

wala jicho kuona

"jicho" lina maana ya kuona kitu. "wala hakuna yeyote aliyeona"

Isaiah 64:5

Taarifa ya Jumla

Watu wa Israeli wanaendelea kuzungumza na Yahwe.

kumbukeni

Hii ni lahaja ambayo ina maana na "kumbuka"

Isaiah 64:6

Taarifa ya Jumla

Watu wa Israeli wanaendelea kuzungumza na Yahwe.

na matendo yetu yote matakatifu ni kama kitambaa cha hedhi

"Kitambaa cha hedhi" ni nguo ambayo mwanamke hutumia wakati wa mwezi anapotokwa damu kutoka kwenye tumbo la uzazi wake. Hii ina maana majaribio yao kumfurahisha Mungu yalishindikana. Sentensi hii ilikusudiwa kushtusha.

Tumenyauka wote kama majani

Isaya analinganisha watu wa Israeli na majaniu ambayo hukauka yanapokufa.

Udhalimu wetu, kama upepo, unatubeba mbali

Hii ina maana dhambi zao, kama jamii, ni sababu ya kushindwa kwao. Isaya analinganisha udhalimu na upepo kama nguvu ya mateso yao ya adhabu ya Yahwe.

umeficha uso wako kwetu

Hii ina maana Mungu alikataa tamaa juu ya watu wake na kuwaacha wateseke.

Isaiah 64:8

Taarifa ya Jumla

Watu wa Israeli wanaendelea kuzungumza na Yahwe.

sisi ni udongo wa ufinyanzi. Wewe ni mfinyanzi; na sisi wote ni kazi ya mkono wako

Hii ina maana Mungu aliwaumba watu wa Israeli.

kumbukeni

Hii ina maana ya kukumbuka kipindi cha nyuma.

tutazame sisi sote

Isaya anamuuliza Yahwe kuzingatia kwa makini hali yao.

Isaiah 64:10

Taarifa ya Jumla

Watu wa Israeli wanaendelea kuzungumza na Yahwe.

Miji yako mitakatifu imekuwa nyika

Hii inasisitiza ya kwamba miji imeangamizwa na hakuna aishiye kule.

Hekalu letu takatifu na zuri, ambapo baba zetu walikusifu, limeangamizwa kwa moto

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Adui ameangamiza hekalu letu takatifu na zuri, pale ambapo baba zetu walikusifu, kwa moto"

Unawezaje kujizuia, Yahwe? Unawezaje kukaa kimya na kuendelea kutudhalilisha?

Wanatumia maswali kuelezea kukata tamaa kwao kwa sababu Mungu bado hajaja kuwasaidia. "Tafadhali usijizuie, Yahwe! Tafadhali usikae kimya na kuendelea kutuaibisha!"

Isaiah 65

Isaiah 65:1

Nilikuwa tayari

Hapa "nilikuwa" ina maana ya Yahwe.

Nimetandaza mikono yangu nje siku nzima kwa watu wakaidi

"Kutandaza nje mikono yangu" ni ishara ya mtu kuonyesha kusihi sana au ombi la nguvu. "Nimeendelea kuwaomba watu wakaidi kupokea msaada wangu"

Isaiah 65:3

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

katika bustani ... juu ya vigae vya matofali

Hii ina maana ya maeneo ya Wakaanani kwa ajilii ya kuabudu sanamu. Madhabahu yao matakatifu yalitengenezwa kwa tofali, ambayo Yahwe alikataza kwa ajili ya madhabahu yake. Madhabahu ya Yahwe ilitengenezwa kwa mawe.

wanakaa miongoni mwa makaburi na kulinda usiku kucha

Hii ni kumbukumbu ya kushauriana na wafu, zoezi ambalo Yahwe alikataza.

wanakula nyama ya nguruwe

Yahwe hakuruhusu watu wa Israeli kula nyama kutoka katika nguruwe.

Isaiah 65:5

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza kwa watu wa Israeli n kuhusu wao.

Mambo haya ni moshi puani mwangu

Yahwe analinganisha watu hawa ambao wanaendelea kumuudhi kwa moshi unaosumbua kupumua kwa mtu.

moto unaowaka siku nzima

Yahwe analinganisha watu wa Israeli kwa moto unaowaka taratibu ambao hutuma moshi bila kukoma huku ikisumbua.

Isaiah 65:6

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza juu ya watu wa Israeli.

Tazama, imeandikwa

"tambua na zingatia kwa makini"

katika mapaja yao

Hii iina maana Mungu atawaadhibu kikamilifu. Msemo huu unalinganisha Yahwe kuadhibu watu kwa kutupa miguu yao wanapokaa.

Isaiah 65:8

Kama pale juisi inavyopatikana kwenye vishada vya mizabibu

Yahwe analinganisha watu wa Israeli kwa kishada cha mizabibu ambacho bado kina juisi nzuri ndani yake.

pale juisi inavyopatikana kwenye vishada

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "utakapokuta juisi katka kishada"

sitawaharibu wote

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya chanya. "Nitawaacha wale ambao ni wa haki"

Isaiah 65:9

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza.

milima yangu

Hii ina maana ya maeneo ya juu kabisa ya Yerusalemu na Yuda yote.

Sharoni

Hili lilikuwa eneo lenye rutuba la malisho.

bonde la Akori

Hili ni jina la bonde ambalo huenda linaweza kukiimbia kutoka Yerusalemu mpaka kusini mwa Yeriko. Hili pia lilikuwa eneo lenye rutuba la malisho.

Isaiah 65:11

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza.

mlima mtakatifu

"Mlima mtakatifu" ni Mlima Sayuni, katika Yerusalemu. "katika mlima mtakatifu wote wa Yahwe"

ambao huandaa meza ... na kujaza vikombe vya divai kwa divai iliyochanganywa

Watu huleta chakula na kinywaji na kuviweka mbele ya sanamu kama sehemu za ibaada yao.

divai iliyochanganywa

divai iliyochanganywa na viungo

Bahati ... Hatma

Haya ni majina ya miungu ya uongo. Pia wanaitwa "Gadi" na "Meni".

Isaiah 65:12

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza kwa wale wa Israeli ambao huabudu sanamu.

amekukusudia kwa ajili ya upanga

"Upanga" inawakilisha silaha za vita ambazo Yahwe atatumia kuafhibu wale ambao hawaitikii wito wa Yahwe.

nilipoita, haukujibu; nilipozungumza, haukusikiliza

Vishazi vyote vina maana moja na vinarudiwa kwa ajili ya msisitizo.

Isaiah 65:13

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza kwa wale wa Israeli ambao huabudu sanamu.

Tazama, watumishi wangu

"Tambua na zingatia kwa makini" Yahwe anarudia hili kwa ajili msisitizo.

lakini utalia kwa sabubu ya maumivu ya moyo, na utaomboleza kwa sababu ya kupondwa kwa roho

Vishazi hivi vina maana moja na marudio ni kwa ajili ya msisitizo.

kupondwa kwa roho

Msemo huu unalinganisha hisia ya kuvunjwa moyo sana na majonzi kwa kitu kuharibika umbo kwa sababu ya shinikizo la juu.

Isaiah 65:15

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza kwa wale wa Israeli ambao huabudu sanamu.

atabarikiwa na mimi, Mungu wa ukweli

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Mimi, Mungu ambaye huzungumza ukweli daima, nitambariki"

shida za awali zitasahaulika ... zitafichwa

Vishazi hivi inaweza kuwekwa katika hali ya kutenda. "watasahau shida zao za awali, kwa maana shida hizi zitatoweka katika kumbukumbu zangu"

zitafichwa kutoka machoni pangu

"kufichwa machoni pangu" inawakilisha uzingatiaji na kumbukumbu ya Yahwe. "Hata sitawaza juu yao tena"

Isaiah 65:17

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza.

Maana tazama

"Tambua! Zingatia kwa makini!"

mbingu mpya na dunia mpya

Tofauti zote ambazo pia huwakilisha kila kitu katikati.

mambo ya awali hayatakumbukwa au kuletwa akilini

Vishazi hivi viwili vina maana moja na zinaungwa kwa ajili ya msisitizo. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "hautafikiria juu ya kile kilichotokea kipindi cha nyuma"

Lakini utakuwa na furaha

Hapa "utakuwa" ina maana watumishi wote wa Mungu.

kutoa machozi na vilio vya dhiki havitasikiwa tena kwake

Unaweza kuelewa hii katika hali ya kutenda. "hakuna mtu atasikia machozi na kulia kwa dhiki tena kwake"

Isaiah 65:20

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza juu ya watu wake waaminifu.

miaka mia moja

"miaka 100"

atachukuliwa kuwa mtu kijana

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "watu watamchukulia kuwa mtu kijana"

atachukuliwa kuwa amelaaniwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "watu watamchukulia mtu huyu kuwa amelaaniwa"

Isaiah 65:22

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza juu ya watu wake waaminifu.

kama itakavyokuwa siku za miti ndivyo zitakuwa siku za watu wangu

"Siku" ina maana ya urefu wa maisha yao. "kwa maana watu wangu wataishi kwa urefu kama miti inavyoishi"

wao ni watoto wa wale waliobarikiwa na Yahwe

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "wao ni watoto wa wale ambao Yahwe amewabariki"

Isaiah 65:24

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza juu ya watu wake waaminifu.

mliima mtakatifu

"Mlima mtakatifu" ni Mlima Sayuni, katika Yerusalemu. "katika mlima mtakatifu wote wa Yahwe"

Isaiah 66

Isaiah 66:1

Mbingu ni kiti changu cha enzi, na dunia ni kigoda cha miguu yangu

Yahwe analinganisha mbingu kwa kiti cha enzi na dunia kwa kigoda cha miguu kusisitiza jinsi alivyo mkuu.

nyumba utakayoijenga kwa ajili yangu iko wapi basi? Sehemu nayoweza kupumzika iko wapi?

Yahwe anatumia maswali kusisitiza ya kuwa wanadamu hawawezi kujenga sehemu kwa ajili yake kuishi.

Isaiah 66:2

Yahwe anaendelea kuzungumza.

Yahwe anaendelea kuzungumza.

Mkono wangu umefanya vitu hivi vyote

"Mkono" ina maana ya nguvu na mamlaka ya Yahwe, sio mwili wa kihalisia.

Tamko la Yahwe

Hii inaweza kuandikwa upya ili kwamba nomino dhahania "tamko" linaelezwa kama kitenzi "kutamka" au "alisema kwa dhati". "hiki ndicho Yahwe wa majeshi alvyotamka" au "hiki ndicho Yahwe wa majeshi alivyosem kwa dhati".

waliovunjika na walio na majuto rohoni

Hapa "kuvunjika" na "kujuta" ina maana ya mtu ambaye ni mnyenyekevu kiukweli na ambaye huteseka kwa ajili ya imani yake.

Isaiah 66:3

Yahwe anaendelea kuzungumza.

Yahwe anaendelea kuzungumza.

Yule anayechinja ... pia hubariki uovu

Vishazi hivi vnne vyote vinafafanua njia tofauti watu waovu wanavyofanya na kufikia maana moja kwa ajili ya msisitizo.

Wamechagua njia zao wenyewe

"Wamechagua kufanya mambo maovu ambayo hukiuka njia za Yahwe"

Isaiah 66:4

Yahwe anaendelea kuzungumza kuhusu watu waovu.

Yahwe anaendelea kuzungumza juu ya watu waovu.

Walifanya kilicho kiovu machoni mwangu

Hapa "machoni" ina maana ya Yahwe kuwachukulia tabia zao. "Walifanya kile nilichochukulia kuwa uovu"

Isaiah 66:5

Na atukuzwe Yahwe

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Mtukuze Yahwe" au "Na Yahwe ajitukuze mwenyewe"

lakini wataaibishwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "lakini nitawatia aibu"

Isaiah 66:6

Yahwe anafafanua adhabu kwa unafiki wa wanaoabudu.

Yahwe anafafanua adhabu kwa unafiki wa wanaoabudu.

Sauti ya ghasia ya vita

Sauti inawakilisha ugomvi wa kweli ambao unaendelea katika hekalu wakati Yahwe anatekeleza adhabu.

Isaiah 66:7

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza.

Kabla hajaingia katika uchungu, anazaa; kabla maumivu hayajaja juu yake, alimzaa mwana wa kiume

Yahwe anazungumza kuhusu Sayuni kana kwamba ilkuwa mwanamke ambaye anataka kuzaa. Ingawa Sayuni iliangamizwa na watu hawakuishi huko tena, Yahwe anaahidi ya kuwa bila kukawia na kwa juhudi kidogo taifa zima litatoka kwake.

Nani amesikia ju ya jambo kama hili? Nani ameona mambo haya? Je! nchi itazaliwa katika siku moja? Je! taifa linaweza kuimrishwa katika muda mmoja?

Yahwe anatumia maswali kusisitiza jinsi tukio hili litakavyokuwa la kipekee. Muendelezo wa maswali unajenga mtanuko hadi Sayuni hatimaye inatajwa.

Isaiah 66:9

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza juu ya Yerusalemu kana kwamba ilikuwa mama.

Je! nitamleta mtoto mchanga karibu na uwazi wa kuzaliwa ... kuzaliwa?

Yahwe anatumia maswali kusisitiza ya kwamba hatashindwa kutimiza ahadi zake kwa watu wa Yerusalemu.

Isaiah 66:10

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza kuhusu Yerusalemu kana kwamba ilikuwa mama na wakazi wa Yerusalemu kana kwamba walikuwa watoto wachanga wapya.

Kwa maana utanyonya na kutosheka; kwa matiti yake utafarijiwa

Hii ina maana Yerusalemu itakuwa sehemu ya usalama na faraja kwa watu wa Mungu. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Kwa maana atakuridhisha kwa maziwa yake; atakufariji kwa matiti yake"

Isaiah 66:12

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza juu ya Yerusalemu kana kwamba ilikuwa mama.

kama mto ... kama kijito kinachomwagikia

Hii ina maana Mungu atasababisha watu wa mataifa kuleta kiasi kikubwa cha utajiri, ambacho kitakuwa cha kudumu kama mto na wingi.

Utanyonya kando yake, kubebwa mikononi mwake, na kuchezeshwa juu ya magoti yake

Hii ina maana Yerusalemu itakuwa sehemu ya usalama na faraja kwa watu wa Mungu.

kubebwa mikononi mwake, na kuchezeshwa juu ya magoti yake

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "atakubeba mikononi mwake na kukurusha juu ya magoti yake kwa furaha"

kwa hiyo nitakufariji, na utafarijiwa Yerusalemu

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "kwa hiyo nitakufariji katika Yerusalemu"

Isaiah 66:14

Maelezo ya Jumla

Isaya anazungumza kwa watu waaminifu wa Mungu.

mifupa yako itachipuka

"Mifupa" ina maana ya mwili mzima kama sehemu yake.

itachipuka kama nyasi laini

"Nyasi laini" huota haraka na kwa imara na hulinganisha na afya na nguvu ya watu waamniifu wa Mungu.

Mkono wa Yahwe utajulikana kwa watumishi wake

Hapa "mkono" una maana ya nguvu yake. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe atadhihrisha nguvu yake kwa watumishi wake"

Isaiah 66:15

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza kwa watu waaminifu wa Mungu.

anakuja na moto

Yahwe kuonekana katika Agano la Kale mara kwa mara huunganishwa na moto ambao huwakilisha hasira ya Yahwe na hukumu.

kama dhoruba ya upepo

Dhoruba inawakilisha matendo yenye nguvu ya Yahwe ya kufanya hukumu yake kuwa na manufaa.

kwa upanga wake

"Upanga" ni silaha ambayo inawakilisha vita zote na mauaji.

Wale watakaouawa na Yahwe watakuwa wengi

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe ataua watu wengi"

Isaiah 66:17

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza.

Wanajiweka wakfu

"Wanajiweka" ni wale ambao huabudu Yahwe lakini wanaenda kinyume na sheria zake.

kuingia katika bustani

Hii ni sehemu ambapo watu wataenda kuabudu sanamu.

yule aliye katikati

Hii inafafanua kionogzi wa wale ambao huenda kuabudu sanamu.

tamko la Yahwe

Hii inaweza kuandikwa upya ili kwamba nomino dhahania "tamko" linaelezwa kama kitenzi "kutamka" au "alisema kwa dhati". "hiki ndicho Yahwe wa majeshi alvyotamka" au "hiki ndicho Yahwe wa majeshi alivyosem kwa dhati"

Isaiah 66:18

Kwa maana mimi ninajua

Hapa "mimi" ina maana ya Yahwe

matendo yao ... mawazo yao

Hapa "yao" ina maana ya wanaoabudu ambao ni wanafiki ambao Yahwe amekwisha wafafanua awali.

Puli ... Ludi ... Tubali ... Yavani

Haya ni majina ya maeneo ambayo yapo mbali kutoka nchi ya Israeli.

Isaiah 66:20

Wataleta

Hapa "wataleta" ina maana ya wageni ambao walisalia na kushuhudia mataifa. Watarudi Yerusalemu na walio uhamishoni wa Israeli.

mlima mtakatifu

"Mlima mtakatifu" ni Mlima Sayuni, katika Yerusalemu. "katika mlima mtakatifu wote wa Yahwe"

Isaiah 66:22

mbingu mpya na dunia mpya

Zote ni utofauti mkubwa mno ambao pia huwakilisha kila kitu katikati.

tamko la Yahwe

Hii inaweza kuandikwa upya ili kwamba nomino dhahania "tamko" linaelezwa kama kitenzi "kutamka" au "alisema kwa dhati". "hiki ndicho Yahwe wa majeshi alvyotamka" au "hiki ndicho Yahwe wa majeshi alivyosem kwa dhati"

Isaiah 66:24

Maelezo ya Jumla

Yahwe anamaliza kuzungumza.

Watatoka nje

Hapa "watatoka" ina maana ya watu wote, waaminifu wa Israeli na wageni, ambao huja kumwabudu Yahwe.

funza ... na moto

Vishazi vyote viwili vinafafanua wazo moja kusisitiza adhabu ya Yahwe.

funza ambazo zinawala

Funza zinawakilisha utisho wa kuoza ambao ni adhabu ya Yahwe kwa waovu.

moto unaoteketeza

Moto pia unawakilisha hukumu ya Yahwe.

hautazimishwa

Hii inaweza kuelezwa kwa chanya. "utachoma milele"

wote wenye mwili

Msemo huu unawakilisha viumbe vyote hai vilivyoumbwa ambavyo hurudi kutoka kwa wafu.

Jeremiah 1

Jeremiah 1:1

Hilikia ... Amoni

majinaya wanaume

Anatothi

jina la mji

Neno la BWANA lilimjia

"BWANA alinena neno lake"

lilimjia

"lilimjia Yeremia"

wa kumi na tatu ... wa kumi na moja

"wa 13...11"

utawala wake

"utawala wa Yosia

pia lilimjia

"neno la BWANA lilimjija"

wa Zedekia

"utawala wa Zedekia"

Jeremiah 1:4

Neno la BWANA lilimjia

Tazama 1:1

lilinijia

"lilimjia Yeremia

sijakuumba

"sijakutengeneza"

Jeremiah 1:7

BWANA asema

"kile ambacho BWANA amesema"

Jeremiah 1:9

nimeweka maneno yangu kinywani mwako

"nimekupa ujumbe wangu ili uwaambie watu

kung''oa

kuvuta mmea kutoka ardhini "kinyume cha kupanda"

kuvunja

kinyume cha kujenga

kuharibu na kutupa

kuangamiza kabisa

Jeremiah 1:11

Neno la BWANA lilinijia

Tazama 1:1

Ninaona tawi la mlozi

BWANA anamuonesha Yeremia maono ya kiroho

mlozi

mti unaotoa mbegu

kwa kuwa ninaliangalia neno langu

Nenol a Kihebarania la "mlozi" na "kuangalia" yanafanana kwa sauti. Mungu anamtaka Yeremeia kukumbuka kuwa anataka neno lake lilitimie kila anapoona tawi la mlozi.

Jeremiah 1:13

Neno la BWANA lilinijia

Tazama 1:1

Jeremiah 1:15

kila mmoja

wale viongozi wa ufame wa kaskazini

atasimika enzi yake katika malango ya Yerusalemu

"atasimamisha hukumu zake kwenye malango ya mji"

nitatamka hukumu dhidi yao

"nitatangaza jinsi nitakvyowaadhibu"

Jeremiah 1:17

Usifadhaike ... nisije nikakufadhaisha

"usiogope sana ... nisije nikakuogofya"

kuvunja

kupasua katika vipande vidogo vidogo

Tazama

"uwe tayari"

chuma ... shaba

zana ngumu zilivyofahamika nyakati zile

BWANA asema

Tazama 1:7

Jeremiah 2

Jeremiah 2:1

Neno la BWANA lilinijia

Tazama 1:1

nijia

kwa Yeremia

Nenda ukanene katiaka masikio ya Yerusalemu

"Nenda ukawaambie watu wa Yerusalemu"

ujana wako

"kwa ajili ya faida yako" au "kwa utashi wako"

tumechumbiana

"tulipokubaliana kwa mara ya kwanza kuwa tutaoana"

katka nchi ambayo ilikuwa haijapandwa

"nchi ambayo hakuna aliyepanda" au "nchi ambayo chakula hakistawi"

BWANA asema

Tazama 1:7

Jeremiah 2:4

nyumbaya ya Yakobo na kila famila katika nyumba ya Israeli

"enyi kizazi chote cha Yakobo"

Ni makosa gani ambayo ... nao si kitu?

"Sikufanya baya lolote kwa baba zenu, kwa hiyo wamenikoseakwa kutonitii na kuanza kuabudu miungu isiyo na kitu chochote na wao kuwa si kchochote!"

si chochote

isiyo na thamani

BWANA yuko wapi, ambaye alitutoa ... Misri? BWANA yuko wapi, ambaye alituongoza ...anayeishi humo?

"Tunapaswa kujifunza kujua kile ambacho BWANA anatutaka kufanya. Yeye ndiye aliyetuleta ... Misri naye ndiya alituongoza ...anayeishi humo."

Jeremiah 2:7

Lakini mlipokuja, mliitia unajisi nchi yangu, mlifanya urithi wangu kuwa chukizo!

Kule mlifanya dhambi na kuichafua nchi nilyowapa!"

Hata makuhani hawakusema . 'BWANA yuko wapi?' na watalaamu wa sheria hawakunijali mimi!

"Makuhani na viongozi wengine wa dini hawakutaka kunifahamu."

BWANA yuko wapi?

"Tunahitaji kumtii BWANA"

Wachungaji wametenda dhambi dhidi yangu

"Viongozi wao wamenitenda dhambi"

wachungaji

"viongozi"

na kuvitafuta vitu ambavyo havina faida

"na kuomba kwa miungu ambayo haiwezi kuwasaidia"

kuvitafauta

"kuitii"

Jeremiah 2:9

Kwa hiyo nitaendelea kuwashitaki

"Kwa hiyo nitaendelea kuwashitaki nyumba ya Israeli"

BWANA asema

Tazama 1:7

watoto wa watoto wenu

"kizazi chenu kijacho"

Kwa kuvuka kwenda hadi pwani ya Kitimu

"kusafiri kwa kuvuka bahari hadi kisiwa cha Kitimu"

Kitimu

Siprusi

Kedari

nchi iliyo mbali mashariki mwa Israeli

Je, taifa limebadilisha miungu ... miungu

"Mtaona kuwa hakuna taifa ambalo limebadilisha ... miungu"

haiwezi kuwasadia

"miungu ambayo haiwezi kuwasaidia"

Jeremiah 2:12

Sitajabuni, enyi mbingu kwa sababu ya hili! Tetemekeni na kuogopa

Msemamaji anageuka na kuziambia mbingu kama vile anaongea na mtu.

wameziacha chemichemi za maji

"wameniacha mimi, chemichemi yao"

kwa kuchimba mabirika kwa ajili yao

"kwa kuabudu miungu isiyokuwa chochote

Jeremiah 2:14

Je, Israeli ni mtumwa? kwani hakuzaliwa nyumbani? kwa nini sasa amekuwa nyara?

"Ninyi watu wa Israeli hamkuzaliwa watumwa; lakini sasa mmetekwa nyara na aduoi zenu."

kwa nini sasa amekuwa nyara?

"Kila kitu mlichomiliki kimechukuliwa kwa nguvu"

Wana simba wameunguruma zdhidi yake ... na kubaki bila watu

"Adui zenu wamewavamia wakiunguruma kama simba. Wameharibu nchi yenu na kuichoma miji yenu. ili kwamba hakuna awezaye kuishi ndani yake"

Wanasimba wameunguruma

"Muungurumo ni sauti kali inayofanywa na wanyama wa wakali"

wakazi

watu wanoishi katika eneo fulani

Nufu na Tahapanesi

Ni miji ya Misri

Watakinyoa kichwa chako

"watafanya kichwa chako kiwe na nyufa"

Je, hamkufanya haya kwa ajili yenu mlipomwacha BWANA Mungu, wakati Mungu wenu alipokuwa akiwaongoza njiani?

"Mmeyasababisha haya ninyi wenyewe kwa kumwacha BWANA Mungu wenu wakati alipokuwa akiwaongoza njiani."

Jeremiah 2:18

Kwa hiyo ... ya Mto Frati?

Msisafiri kwenda Shihorikufanya ushirika na watawala wa Misri. Msisafri kwenda Frati kufanya ushirika na Ashuru!

Shihori

Ni mpaka wa Kanaani uliio kusni magharibbi ya Kanaani, kwenye mto uliokauka.

Uovu wako unakukukemea na maasi yako yatakuadhibu.

"Kwa sababu umekuwa mwovu na mwasi, Nitakuadhibu."

ni uovu na uchungu

"ni uovu uliokithiri"

hofu

hofu kuu

Jeremiah 2:20

Kwa kuwa nilivunja nira yenu mliyokuwa nayo wakati wa kale; Nilivichana vifungo vyako kutoka kwako Lakini bado ulisema, 'Sitamtumikia!'

"Hapo zamani niliwakomboa kutoka utumwani, lakini mlikataa kuniheshimu mimi!"

tangu ulipopiga magoti katika kila kilima na kuusogelea kila mti wenye majani mabichi, enyi makahaba.

Mlizipigia magoti sanamu na kuziabudu kama mwanamke mzinzi anavyomfanyia mume wake"

Vifungo

ni minyoror inayotumika kumfunga mtu au mnyama

kusogelea

kuwa chini

Lakini mimi mwenyewe niliwapanda kama mzabibu, mbegu iliyokamilika.

Mimi, BWANA, ndiye nilikuanzisha kwa mwanzo mwema."

niliwapanda

kuweka kwenye ardhi ili kukua

na kuwa mzabibu usiofaa na mzabibu pori

"umekuwa kama maozea, divai isiyofaa"

usiofaa

msaliti, mwasi

dhambi yako ni madoa

"bado una hatia ya kutenda dhambi

madoa

madoa yanawakilisha ukumbusho wa mara kwa mara wa dhambi ya Waisraeli

Asema BWANA

Tazama 1:17

Jeremiah 2:23

sijaeanda

"sijaabudu"

Tazama tabia zako zilivyokuwa bondeni! ...njia yake!

"Lazima uyatazame matendo uliyofanya katika bonde nje ya Yerusalemu. Unakimbia mbele na nyuma ukifukuza huyu na yule kama ngamia mwepesi asiyejua kule anakoelekea."

mwepesi

"kasi" au " haraka"

Wewe ni punda wa mwitu .... wakatai wa mwezi wa kupandwa

"Wewe ni kama punda jike mchanga anapokuwa katika wakati wa kupandwa huwa hawezi kujizuia na mara kwa mara hubadilishi maeneo akitafuta dume la kumpanda. Punda dume wala hawafukuzi kwa sababu punda jike hujipeleleka,"

anapotafuta

"tamaa kali"

avutaye pumzi za upepo

"kupumua kwa nguvu na kwa haraka"

Lazima uizuie miguuyakoisikose kiatu ... huwatafuta

"Nimekuambiauache kukimbiakimbia hapa na pale ukimbilia Miungu ya uongo, kwa sababu matokeo yakae ni kumaliza viatu n akukufanya uwe na kiu. Lakini unaniambia, 'Hatuwezi kujizuia. Lazima tuifuate hii miungu ya Baali na kuiabudu!"

kiu

hitaji lamaji

wageni

watu ambao hatujawahi kukutana nao

Jeremiah 2:26

anapokuwa amekamatwa

"anapokamatwa"

wao

"watu"

hawa ndiowale waiambiayo miti, ninyi ndi baba zangu; na mawe, 'ninyi ndio mlionizaa,'

"hawa ndio watu wanaoimbia miti iliyochongwa, "ninyi ndio baba zangu," na mawe yaliyochongwa, :ninyi ndio mlionizaa." "

kwa kuwa migongo yao hunitazama na siyo nyuso zao

"hugeuka na hawaniabudu" au "hugeuka na kwa hiyo mimi huona migongo yao tu, wala si nyuso zao."

Amka utuokoe

"BWANA njoo utuokoe."

Jeremiah 2:29

Kwa nini kunituhumu kwa kufanya makosa? Ninyi nyote mmeniasi

"Ninyi Israeli mnadai kuwa mimi nilikosea pale niliposhindwa kuwaokoa mliponiita, hata kama mnaendelea kunitenda dhambi."

umewaangamiza

"uko tayari kuleta maangamizi makubwa"

Enyi watu wa kizazi hiki! Sikilizeni neno langu, neno la BWANA

"Enyi nyumba ya Yuda, silikizeni neno ninalowaambia."

Je, nimekuwa jangwa kwa Israeli? Au nchi yenye giza nene?

"Sikuwatelekeza jangwani wala kuwaacha kwenye nchi yenye giza nene"

Kwa nini watu wanguhusema, 'Acha tuzungukezunguke hatutakuja kwako tena'?

"Kwa niin masema, "Tunaweza kwenda kule tutakako kwenda na wala kumwabudu BWANA tena.'

Jeremiah 2:32

Je, mwanamwali anaweza kusahu mapambo yake, na bibi arusi mavazi yake?

"BWANA anaanza kuwakemea watu wake kwa kumsahau"

kwa siku nyingi

"muda mrefu sana"

Jinsi mlivyotengeneza njia zenu vizuri ili kutafuta mapenzi. Hata mmewafundisha njia zenu wanawake waovu,

BWANA anasema kuwa Waisraeli wamekuwa wazuri wa kutafuta miungu ya uongo kiasi kwamba wanaweza kumwosha kahaba namna ya kuwakaribisha wateja.

Damu ambayo ilikuwa ndio uhai wa watu wasio na hatia, imeonekana katika mavazi yenu

Mnahatia ya kuwaua watu masikini na watu wasiokuwa na hatia, watu ambao hawakufanya chocote kuwaumiza."

Hawa watu hawajawahi kuonekana katika matendo maovu.

"Hmkuwaona hawa watu watu wakiiba"

Jeremiah 2:35

Mimi

"sisi"

Kwa hakika hasira ya BWANA itageuka kutoka kwangu

"Kwa hakika BWANA hatakuwa mwenye hasira tena

utahukumiwa

"utakukumiwa vikali"

Tangu

"kwa sababu"

sikutenda

"hatukutenda"

kwa nini mnatangatanga kwa urahisi katika njia zenu

BWANA anawatania Waisraeli kwa sababu ya kubadilisha kutoka ufame mwingine hadi mwingine kutafuta msaada lakini hawakumtegemea Mungu kwa ajili ya kupata msaada

kwa urahisi

bila kujali

mmehuzunika

kujisikia kuwa na huzuni au kutokuwa na furaha kwa sababu mfalme wa Misri alikataa kuwasaidia.

Mtaondoka hapo mkiwa

"Mtaondoka hapo kutoka Misri"

mmehuzunika

kwa huzuni kwa sababu hamkupata msaada wa Wamisiri.

mikono vichwani mwenu

Hii inaonesha watu wakiwa katika maombolezo

Jeremiah 3

Jeremiah 3:1

Taarif kwa ujumla

BWANA bado anaendelea kuongea kama ilivyokuwa kwenye sura 2

Je, huyo si najisi kabisa

"Ni najisi kabisa"

Huyo mwanamke ndiyo hii nchi

Nchi hii ni kama huyo mwanamke

Mmetenda kama kahaba

Mmetoa upendo wenu kwa sanamu ka vile kahaba atoavyo mwili wake kwa mwanamume ambaye si mume wake"

na sasa mnataka kurudi kwangu tena

"Sitawapokea tena kama mtajaribu kurudi tena kwangu."

Asema BWANA

Tazama 1:7

inua macho yako

"Tazama juu"

Je, kuna mahali ambapo hukufanya ukahaba?

"Wewe ni kama mwanamke ambaye huenda kila mahali na wanaume humkamata na kulala naye

Mwarabu

gege la wanyang'anyi

Jeremiah 3:3

mwanamke kahaba

anayelala na wapenzi wengi

Tazama

"sikiliza kwa makini"

Jeremiah 3:6

Yeye anaenda

Watu wa Israeli huenda

kila kilima na katika kila mti wenye majani mabichi,

Juu ya viliima na chini ya miti yenye vivuliilikuwa nia maeneo kwa ajili ya kuabudia

Kisha dada yake ambaye ni mwasi

"Watu wa Yuda, ambao pia hawakunitii"

Jeremiah 3:8

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kuongea

Israeli aliyeasi

Ewe Israeli, umeaacha kabisa kunitii"

mwenye hana

"asiyestahili"

Asema BWANA

Tazama 1:7

Jeremiah 3:11

mwenye haki, haki

Neno "haki" na "mwenye haki" linamlenga Mungu ambaye yeye ni mwema, mwenye hukumu sahihi, mwaminifu, na mwenye upendo, na kwa sabab yeye ni mwenye haki; basi ataihukumu dhambi.

Neno

Neno linamaanishsa kitu ambacho mtu amesema.

mwaminifu

Kuwa mwaminifu kwa Muungu maana yake ni kuishi kulingana na mafundisho ya Mungu.

Jeremiah 3:13

Wachungaji niwapendao

Wapendao kile ninachopenda

Jeremiah 3:16

utaongezeka nakuzaa maatunda

"Utatongezeka sana kwa idadi"

Jeremiah 3:17

Nyumba ya Yuda itaishi na nyyumba ya Israeli

"Watu wa Yuda wataishi pamoja na nyumba ya Israeli.

Jeremiah 3:19

Lakini mimi

Neno "mimi" linamaanisha BWANA

kukuheshimu kama mwangu ... kama mwanamke

Mabadiliko haya ya kutoka kwa mwanmume kwenda kwa mwanamke ni kwa ajili ya msisitizo mkubwa.

Asema BWANA

Tazama 1:7

Jeremiah 3:21

Sauti ilisikika

"Watu walisikia sauti"

Kilio na kusihi

"kulia kuomba kwa sauti ya juu"

Tazama

Neno "tazam"a hapa linatupa angalizo la kusikiliza kwa makini kwa ajili ya taarifa za kushangaza zinazofuata.

Jeremiah 3:23

Uongo hutoka kwenye vilima

Watu hutegemea mwongozo na kutoka kwenye ibaada za sanamu lakinni huambulia uongo

Na tulale chini kwa aibu. Aibu yetu na itufunike

"Acha tuaibike kabisa"

Wakati wa ujana wetu

"kuanza kwa taifa"

Sauti ya BWANA

"kile ambacho BWANA asemacho"

Jeremiah 4

Jeremiah 4:1

Kama utarudi, Israeli

"Kama utanirudida, au kama mtabadilisha tabia zenu, enyi watu wa Israeli"

ikiwa kwangu kwamba umerudi.

"kisha ukaanza kuniabudu"

Asema BWANA

Tazama 1:7

Kama utaondoa hayo mabao yachukizayo mbele yangu

"Ondoa hizo sanamu zichukizazo mbele yangu"

na ukaacha kunikimbia mimi tena

"ukabaki mwaminifu kwangu"

Limeni shamba zenu na msipande kwenye miiba

BWANA anawaambia watu wake kuandaa maisha yao kama mkulima aandavyo shamba kwa ajili ya kupanda

Jeremiah 4:4

Mtahiriwe kwa BWANA nakuondoa goviza mioyo yenu

"Mjitoa kikamilifu kwa BWANA"

Mtahiriwe kwa BWANA

"Tahiriweni kwa BWANA"

hasira yangu itawaka kama moto

"vitu ambavyo nafanya kwa sababu nina hasira vitakuwa kama moto

Waambie Yuda na Yerusalemu isikie

"wafanye watu wa Yerusalemu wasikie"

na Yerusalemu isikie

"ifanye Yerusalaemu isikie"

majanga ... angukokubwa

"anguko kubwa" inaeleza jinsi janga litakavyokuwa

kutokea kaskazini

jeshi la adui litatokea kaskazini

Jeremiah 4:7

Simba anakuja

"jeshi lenye nguvu na kali linakuja"

kichaka

ni jumla ya mimea inayokua pamoja

ameanza kuja

"ameanza kusogea"

hofu

kuogopa, kutetemeka

lieni

kilio cha sauti na na huzuni na toba kwa sababu ya kutenda dhambi

Jeremiah 4:9

Asema BWANA

Tazama 1:7

upanga unawaangukia dhidi ya maisha yao

"adui zetu wako tayari kutuchinja kwa panga zao"

Jeremiah 4:11

itasemwa

"BWANA atasema"

Upepo uwakao kutoka katika nyanda ... upepoulio na nguvu

Moto na adui asiyekuwa na msamaha anakuja

binti wa watu wngu

Taifa limelinganishwa na bibi arusi maalumu katika mahusiano ya kimahaba

Hautapepetwa wala kuwatakasa

"sitaziondoa dhambizao"

Upepo ... utakuja kwa amri yangu

"Upepo huo utaamriwa na Mungu kuja.

kwa amri yangu

"kutoka kwangu"

sasa napitisha hukumu dhid iyao

"natangaza hukumu"

Jeremiah 4:13

Tazama anavamia kama wingu, na magari yake ni kama dhoruba

"jeshi la adui ni haribifu kama upepo mkali"

Ole wetu kwa kuwa tutaharibiwa

"Watu wanasema, 'kwa hakika tutaangamizwa.'"

Itakaseni mioyo yenu kutoka uovu wenu

BWANA anawaambia watu waishio Yerusalemu, '"Bora mbadilishe tabia zenu."

kuna sauti iletayo

"wajumbe wanahubiri"

na janga lijalo linasikikka

"watu walilisikia hilo janga"

kutokea Dani ... milima ya Efraimu

watu walitambua kuwa wale watu waliokuwa wakitangaza onyo hili walikuwa wanakaribia

Jeremiah 4:16

Watakuwa kama walinzi wa shamba lililolimwa pande zote

"watauzingira mji wote"

Asema BWANA

Tazama 1:7

Itakupiga moyo wako

"itapiga kila kitu ukipendacho"

Jeremiah 4:19

Moyo wagu! moyo wangu! Niko katika maumivu ya moyo. Moyo wangu umefadhaika ndani yangu.

"Niko katika maumivu makali, Nimezidiwa"

misukosuko

kuchanganyikiwa

Anguko baada ya anguko limetangazwa

"watu wanaambizana kutoka mji mmojahadi mwingine kuwa wameharibiwa"

nchi yote imeharibiwa mara

"adaui wameiharibu nchi"

masikani yangu na hema yangu

neno "maskani" na "hema" yanamaanisha kitu kimoja. Maana yake yaweza kuwa "hema yangu na mapazia yaliyo ndani yake" au "mahali niishipo"

Jeremiah 4:21

Vita hivi vitaendelea mpaka lini? Ni mpaka lini nitasikiliza sauti za pembe?

"Natamani kama hivi vita vingeisha haraka"

watu wajinga

watu wapumbavu"

Jeremiah 4:23

Niliiona nchi, na kuiona

Huu ni mwaliko kwa Yeremia kuyatazama maono ambayo Mungu anampatia

ilikuwa ukiwa na utupu

Huu ni unabiiwa jinsi nchiya Israeli it akavyokuwa baada ya watu wote kupelekwa katika utumwa.

Tazama

Neno "tazama" linatuashiria kuwa tayari ili kupokea taarifa zinazofuata

Jeremiah 4:27

nchi itaomboleza, na mbingu kule juu itatiwa giza

Yeremia anasisitiza hukumu ya BWANA kwa kusema kuwa dunia yote pia inaonyesha huzuni yake.

Kila mji utakimbia ... kila mji utapanda

Huu ni msisitizokuwa watu wote watakuwa wakikimbia.

Miji itatelekezwa, kwa kuwa hakutakuwa na mtu wa kuishi katika miji hiyo

"hakutakuwa na mtu atakayebakizwa katika hiyo miji"

Jeremiah 4:30

unavaa mavazi mekundu ...mapambo ... macho ... ya maumivu

"unavaa kama kahaba"

mapambo

"kujipamba" au "kuongeza vitu vinavyomfanya mtu avutie au aonekane wa gaharam zaidi"

wanaume waliokutamani sasa wanakukataa

Hii inasisitiza kuwa mataifa mengine ambayo Israeli alwataegemea kwa utajiri na biashara sasa watamkataa watakapaoiona hukumu ya Mungu.

Utungu kama wa mwanamke

"huzuni na utungu kama wa mwanamke anoupata wakati wa kujifungua"

Atwetaye

"uhai wangu umechanika kwa sababu ya huzuni"

Jeremiah 5

Jeremiah 5:1

Taarifa kwa ujumla

Yeremia anawaambia atu wa Yerusalemu.

Kimbieini mkapite

"Fanyeni haraka"

kama mtaweza kumpata

"tazameni mkatafute"

viwanja vayke

eneo wazi kubwa ambapo watu hukusanyika

kama mtaweza kumpata hata mtu mmoja

"kama mtapata hata mtu mmoja"

anayetenda kwa haki

"anayefanya kile kilicho sahihi"

hata kama wana

Kiwakiishi "wa" kinawakilisha watu wa Yerusalemu

Kama BWANA aishivyo

Tazama 4:1

macho yako hayatazami uaminifu

"unataka watu wawe waaminifu"

unawapia watu, lakini hawasikii maumivu

"unawaadhibu watu lakini bado, hawasikii"

umewaangamiza kabisa

"umewateketeza kabisa"

kuwa waadilifu

"kujifunza"

Wanafanya nyuso zao kuwa ngumu kama mwamba

"wanakuwa wasumbufu sana"

Jeremiah 5:4

Kwa hiyo nilisema

"Yeremia anaongea

Lakini wote wanvunja nira yao pamoja; wote wanaivunja ile minyororo inayowafunga kwa ajili ya Mungu.

Nira na minyororo inawakilisha sheria inamfunga mtu na Mungu wake.

Kwa hiyo simba ... mbweha ... chui ..

maana yake yaweza kuwa 1) "Wanyama wa mwituni wakuja na kuwaua watu" au 2) "jeshi la adui litkuja na kuwaua watu"

kichaka

ni miti mingi ambayo imekwa kwa pamoja na iko karibu

mbweha

"mbwa mwitu"

anawasubri

anasubiria

chui

mnyama wa mwitu mkali

hayana ukomo

yasiyoweza kuhesabika

Jeremiah 5:7

kwa nini niwasamehe hawa watu

"Kwa sababu ya mambo wanayofanya, siwezi kuwasamehe hawa watu"

hwa watu

Watu wa Yerusalemu

awana wenu

watu wa Yerusalemu

Niliwalisha vya kutosha

"Niliwapatia kila kitu walichohitaji"

na kuchukua alama za nyumba za uzinzi

"na kwenda katika makundi makubaw kwenye nyumba za uzinzi"

katika joto

"aliye tayari kupandwa"

kupandwa

wakati wanyama wanapolala pamoja ili kuazlisha

Kila mume alimkaribia mke wa jirani yake

"kila mwanume alikuwa anajaribu kulala na mke wa jirani yake."

kwa hiyo kwa nini nisiwaadhibu ... na kwa nini nisijilipizie kisasi juu ya taifa kama hili

"Kwa sababu wanafanya mambo haya, Nitawaadhhibu ... kwa hakika lazima nilipe kisasi changu dhidi yao."

Asema BWANA

Tazama 1:7

Jeremiah 5:10

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kuongea

Nenda hadi kwenye shamba lake la mizabibu

Pandeni juu ya kuta zake. "BWANA anaulinganisha mji wa Yerusalemu na na shamba la mizabibu ambao una ukuta unaozunguka.

Panden juu

BWANA anawaambia adaui za watu wanaoishi Yerusalemu

msiwaharibu kaisa

"msiiwaangamize kabisa"

Ondoeni matawi kwa sababu hayatoki kwa BWANA

"Waondoeni watu wote waovu kwa sababu hawatoki kwa BWANA"

Kwa sababu ya nyumba za Yuda na Israeli

Kwa ajili ya watu wa Israeli na Yuda

Asema BWANA

Tazama 1:7

wamenikataa

"wamedanganya juu yangu"

Yeye si halsi

"Hawezi kufanya mambo haya

Maovu ahayawezi kutupata, wala hatutaona upanga wala njaa

Virai hivi viwili vunaongelea jambao moja tu, jamabo la pili liko wazi zaidi kuliko la kwanza.

wala hatutaona upanga wala njaa

"hatutakuwa na vita wala njaa"

Jeremiah 5:14

Kwa sababu ume

Kiwakilshi cha "u" kinawakilisha watu wa Israeli

asema hivi

Tazama 5:10

tazama

"Sikiliza"

nataka kuweka maneno yangu kwenye kinywa chako.. Yatakuwa kama moto

"Nataka kutengeneza maneno amabyo wewe utayasema kwa kwa niaba yangu kwa moto"

katiak kinywa cahcako

kiwakilishi cha "chako" kinamaanisha Yeremia."wewe uyaseme"

watu hawa

watu wa Israeli

kwa kuwa utawaramba

Kwa sababu utawaharibu watu wa Israeli utakaposema maneno yangu."

dhidi yenu

"kuwashambulia ninyi"

nyumba ya Israeli

Tazama 2:4

ni taifa linalodumu, ni taifa la kale!

ni taifa la miaka mingi na lenye kuvumilia

ni taifa ambalo lugha yake hamuijui, wala hamutaelewa wasemacho

"Ni taifa ambalo lugha yake hamutielewa."

Jeremiah 5:16

Podo lao ni kaburi wazi

"Taifa hili litatumia mshale kuuwa watu wengi sana"

Podo lao

neno "lao" inawakilisha taifa ambalo BWANA atalileta kuwangamiza Waisraeli.

podo

"chombo cha kuwekea mishale"

kwa hiyo mavuno yako yataliwa

"Kwa hiyo jedshi la taifa hlo litakula kile mnachotegemea kuvuna"

Watakula

kiwakilishi cha "wa" kinamaanisha jeshi la taifa lile.

Waiangusha chini kwa upanga miji yenu na boma zake

Watatumia silaha zao kuingamiza miji yenu"

ambazo mnazitumainia

"ambazo mnadani kuwa ziko imara kuwalinda"

Jeremiah 5:18

katika siku hizo

Kirai "siku hizo" kinamaanisha wakati ambapo hilo taifa litakuja kuwavamia watu wa Israeli.

asema BWANA

Tazama 1:7

sikusudii kuwaharibu

"sitawaangamiza"

itatokea kwenu

"itakapotokea kwamba .."

haya yote

BWANA atatuma jeshi geni kuiangamiza Israeli.

kuabudu miungu migeni

"kuwatumikia miungu migeni"

Jeremiah 5:20

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaongea na watu wa Israeli.

Waambie haya

"sema haya"

nyumba ya Yakobo

Tazama 1:7

yasikike katika Yuda

"yatangaze katika Yuda"

watu wapumbavu! Sanamu hazina matakwa

"watu ambao hawawezi kuelewa"

zina amaaaacho lakiniahaziwezi kuona.

"mna macho lakini hamwezi kuelewa ninachofanya"

zina masikio lakiini haziwezi kusikia

"mna nasikio lakiini hamuelewi kile ninachowaelezeni"

asema BWANA

Tazama 1:7

Je, hamnihofu mimi

"ni upumbavukwamba hamnihofu...uso

au kutetemeka mbele ya uso wangu

"kutetemeka kwa hofu kwa sababu yangu"

Nimeweka mpaka wa mchanga kwenye bahari

"Niliweka mchanga kuwa mpaka wa habari"

ni agizo la kudumu ambalo halibomoki

"ni ukomo wa kudumu ambao hauwezi kuvukwa"

kupwa na kujaa

"huinuka juu na kurudi chini"

hayawezi kuvuka

"hayawezi kufanikiwa kuvuka mpaka"

Jeremiah 5:23

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kuwaambia wana wa Israeli.

mioyo ya usumbufu

"ni msumbufu na mpinzani"

Hugeuka kuwa wapinzani na kuondoka

"hawatii wala kusikliza."

hawasemi mioyoni mwao

"hawafikirii wao wenyewe"

ambaye hutunza majumaya mavuno ka ajili yetu

"nakuhakikisha kwa ajili yetu kuwa majuma ya mavuno yawepo kwa wakati wake"

uovu wako

Neno "wako" linamaanisha kizazi chaYakobo na watu wa Yuda. "dhambi zako"

mambo mema

mvua na mavuno

Jeremiah 5:26

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaenedelea kuongea

watu wao wamo kati ya watu wangu

"kwa kuwa nimewaona watu waovu kati ya watu wangu

wanaweka mtego na kukamata watu

"wanapanga vitu ili kwamba wapate nafasi ya kupata watu"

wanakua na kutajirika

"wanakuwa na nguvu pia matajiri"

wanang'aa nakupendeza

"wana ngozi laini na wene kupendeza"

wamepitiliza hata mipika ya maovu

"wanafanya vitu ambavyo viko zaidi ya uovu"

Sababuy a kuwepo kwa watu yatima

"hawawajali kusadaia mashauri yanayoletwa na yatiima

kwa nini nisiwaadhibu ... taifa la namna hii

Tazama 5:7

Jeremiah 5:30

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kuongea

Jambo la ajabu la kuchukiza limetokea

"Jambo la kuogofya na la kusikitisha limetokea"

katika nchi hii

"katika nchi ya Israeli"

Manabii wanatabiri kwa uongo

"wanatabiri uongo"

wanatawala kwa masaada wao

"kutokana na uongozi wa manabii"

lakini mwisho kitatokea nini?

lakini utakuwa katika tabu na majuto kwa sababu ya tabia hii ya uovu itakapoishia kuhukumiwa?"

mwisho

neno "mwisho" linamaanisha adhabu ambayo ni matokeo ya uovu ambao watu wamefanya"

Jeremiah 6

Jeremiah 6:1

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaongea

Tafuteni mahali salama

"iweni wakimbizi"

Pigenji tarumbeta

"enyi watu mnaoishi katika mji wa Tekoa jiandaeni kuangamizwa"

Tekoa

hili ni jinala mji ulio kilomita 18 kusini mwa Yerusalemu. Maana ya jina ni "pembe la kupuliza"

Simamisheni ishara juu ya Beth-Hakeremu,

"Enyi watu mnaoishi katika mji wa Beth-Hakeremu; jiandaeni kuzingirwa"

Beth-Hakeremu

Hili nij ina mji ulio kilomita 10kusini mwa Yerusalemu. Jna linamaanisha "mahali pa mizabibu."

ishara

"ishara ya kuwaonya watu kuwa kuna inakuja

kwa uovu unaoonekana

"kwa kuwa watu wanona kuwa kuna janga linalokuja"

pigo kubwa linakuja

"maangamizi makubwa"

Binti za Sayuni, warembo na mwororo

"Binti za Syuni ambao ni kama warembo na mwororo"

Binti za Sayuni

Tazama 4:30

wachungaji na kondoo wao watawaendea

"Wafame na wanajeshi wataizingira Yerusalemu

zikiwazunguka pande zote

"karibu naye pande zote

kila mtu atachunga kwa mkono wake

"kila mfalme ataangamiza akiwa na askari wake"

Jeremiah 6:4

Taarifa kwa ujumla

Mflame toka jeshi litaloangamiza anaongea na wanaume walio chiniya mamlaka yake.

Jitakaseni wenyewe kwa miungu kwa ajil ya vita

"Jiandeni kwa vita kwa kujitakasa na kutoa sadaka kwa miungu"

Twendeni

"inukeni"

adhuhuri

"adhuhuri bila kujali kuwa joto ni kali"

mchana unatoweka

"mchana unafika mwisho

vinakuja

"vinachomoza"

usiku

"wakati wa usiku hata kama kuna giza"

ngome zake

"majengo imara ya Yerusalemu"

Jeremiah 6:6

Kateni miti yake

"Ikateni miti yake" BWANA anawaambia lile jeshi ambalo litaivamia Yerusalemu.

vifusi vya kuitekea

"vifus." Hivi ni vifisi vya takataka ambavyo vitawawezesha wanajeshi kuziangamiza kuta za Yerusalemu

kwa sababu umejaa ukandamizaji

"kwa sababu watu wake wanaoneana wao kwa wao"

Kama vile kisima kitoavyo maji, vivyo hivyo mji huu uzaavyo uovu

Kama vile kisima kinavyobaki na maji, Yerusalemu imebaki na uovu, hata kama BWANA anaiadhibu.

uharibifu na jeuri vimesikika kwake

"Ninasikia uharibifu na ujambazi kwake."

Mateso na jeuri viko mbele yangu daima

Daima ninaona ugonjwa na mateso."

Uadhibishwe, ee Yerusalelmu

"Jifunzeni kutoka kwenye hiyo adhabu yenu, enyi watu wa Yerusalemu.

nchi isiyokariwa na watu

"nchi ambayo hakuna watu wanaoishi ndani yake"

Jeremiah 6:9

Hakika wataokota mabaki ya Israeli waliobaki kama zabibu

"Watarudikuwaangamiza Waisraeli waliobaki Israeli baada ya kuwa wamewaanagamiza."

Hakika wata

Kiwakilishi "wa" kinawakilisha lile jeshi ambalo BWANA analituma kuiangmiza Israeli.

Nyosha mkono wako

BWANA anaongea na adaui wanaowangamiza Israeli.

Nyosha mkono wako ili uchume Zabibu

"Njoni muwaangamize Waisraeli."

Nitamwambia nani

Yeremia anaongea

Nitamwambaia nani na kumwonya nani ili wasikilize

"Hakunaaliyebaki kwangu wa kumwambian a kumwonya ili anisikilize."

Tazama

BWANA anatumia neno hili "tazama" ili kusisitiza anachokisema.

Masikio yao hayakutahiriwa

"Wanakataa kusikiliza" au "Wanakataa kutii"

Masikio yao

"Kiwakilishi "yao" kinamaanisha Waisraeli.

Jeremiah 6:11

Lakini nimejazwa

Anayeongea na Yeremia

nimejazwa na hasira za BWANA

"nina hasira sana pamoja na BWANA."

Nimechoka kuizuia

"Nimechoka kutoisema hasira ya BWANA"

Imwage mbele ya watoto mitaani

"watoto mitani" inamaanisha watoto wote katika mji. "Iseme hasira yangu kwa watoto wa mji"

Kwa kuwa kila mume atachukuliwa pamoja na mke wake

"Kwa sababu adui watakamata mume na mke wake."

kila mzee mwenye miaka mingi

"mwenye miaka mingi" inamaanisha "mzee sana" "kila mzee sana"

watapewa watu wengine

"itakuwa mali ya mtu mwingne"

mashamba yao na wake zao pamoja

"mashamba yao na wake zao pamoja"

Kwa kuwa nitaangamiza wakazi wa mji kwa mkono wangu

"Kwa kuwa nitatumia nguvu zangu kuwaangamiza watu wanaoishi katika nchi"

asema BWANA

Tazama 1:7

Jeremiah 6:13

kutoka kwa mdogo hadi kwa mkubwa

"watau wote wa Israeli waliobaki kutoka kwa mtu dahaifu kabisa hadi mwenye nguvu."

anatamani mapato ya udanganyifu

"anayefanya mambo mabaya kwa wengine ili apate fedha"

vidonda vya watu wangu

"matatizo makubwa amabayo watu wangu wanayo"

kwa juu juu

"kama vile havikuwa vinvauma"

'Amani! Amani! na kumbe amani haipo

"Yote yako sawa! kumbe hayako sawa"

Je, waliona aibu walipofanya machukizo?

"Walifanya dhambi mbaya sana, lakini hawakuna aibu"

Hawakuona aibu, hawakuwa na aibu

"hawakuona aibu kwa kile walichofanya"

wataanguka

"watauawa"

wataangushwa

"watajikwaa" au "watapoteza nguvu zao na kuwa dhaifu"

Jeremiah 6:16

Simama kwenye njia panda

BWANA anaongea na watu wa Israeli.

Simama kwenye njia panda ...Htutaenda

Haya mabarabara na njia inamaanisha aina ya maisha ambyo watu wanaishi. BWANA anataka watu wa Israeli waulize aina ya maisha mazuri kwao kuishi.

uliza njia za zamani

"uliza mababu zao waliishije"

Niliweka walinzi juu yenu ... Hatutasikia

BWANA anawaeleza manabii kama walinzi ambao walitumwa kuwaonya watu katika hatari.

niliwaweka.. juu yenu

Kiwakilishi "yenu" kinamaanisha Israeli

wasikilize tarumbeta

"kusiliza sauti za tarumbeta" BWANAanawaamuru watu wasikilize maonyo ambayao aliwapatia kupitia kwa manabii.

Kwa hiyo, sikilizeni, enyi mataifa! Tazamaeni enyi mashahidi, muone kile kitakachowapata. Sikia wewe dunia, Tazama.

Virai hivi vitatu vyote viinawaambia watu wa mataifa mengine kushudia kile ambacho BWANA atafanya kwa hili taifa pinzanij la Yuda.

Niko tayari kuleta janga kwa watu hawa

"kwa haraka nitawaadhibu watu hawa"

enyi mashahidi

"enyi ambao mtashuhudia"

kitakachowapata

"neno "wa" linamaanisha watu wa Israeli.

sikia wewe, dunia

"Sikia, watu wanaoishi katika dunia."

matunda ya fikra zao

"janga ni matokeo ya fikra zao."

Hwakusikiliza neno langu wala sheria zangu badala yake walizikataa.

"Hawakusikiliza nilichowaambia kufanya"

Jeremiah 6:20

Huu ubani unaopanda kutoka Sheba una maana gani kwangu? au huu udi kutoka nchi ya mbali?

Sihitaji ubani kutoka Sheba au harufu nzuri ya mafuta kutoka nchi ya mbali?

huu udi

Hii harufu nzuri ilitumiKa kumwabudu Mungu hekaluni

hazikubaliki kwangu

"havinifurahishi"

Tazama

neno "tazama" hapa linaongeza msisitizo kwa kile kiinachofuata, "kwa kweli"

Niko tayari kuweka kikwazo dhidi ya watu hawa

""Niko tayari kuweka kikwazo mbele ya watu hawa"

kikwazo

magumu

juu yake

"juu yao"

baba na watoto wao

"baba na watoto wote watajikwaa"

wakazi na jirani zao

"majirani na marafiki"

limechochewa kutoka nchi ya mbali

"limehuhishwa ili lije kutoka maeneo ya mbali"

Jeremiah 6:23

Watachukua

"Watashikilia" kiwakilshi cha "wa" kinamanisha wale wanajeshi wale watakaotoka kasazini.

Sauti zao ni kama muungurumo wa bahari

"sauti ile wanayoifanya ni ya muunagurumo mkali kama ya bahari

katika mfumo wa wanaume wa vita

"lile jeshi limejipanga vizuri ili kwamba wale wanaume waingie vitani"

enyi binti wa Sayuni

Tazama 4:30

Tumesikia

Kiwakilishi "tu" yawezekana kinamwakilisha Yeremia akiongea na watu wote wa Yuda.

inalegea kwa dhiki

"imelegea kwa sababu tuna mashaka"

maumivu yametukmata

"Tuko kwenye maumivu"

kama utungu wa mwanamke

"kama mwana mke anayezaa"

Jeremiah 6:25

Taarifa kwa ujumla

Hii yawezekana BWANA anaongea na binti wa Yerusalemu wanaowakilisha watu wote w a Yerusalemu

Binti za watu wangu

Tazama 4:11

jivikeni magunia nakugaagaa kwenye majivu ya ya maombolezo ya mwana pekee.

"iweni wenye huzuni"

kwa kuwa anayewaangamiza anakuja kwetu ghafla juu yetu

"kwa sababu jeshi la adui linakuja ghafla kutuangamiza"

Jeremiah 6:27

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaongea

kuwajaribu watu wangu kama mtu anyepima fedha.

"mtu atakayewapima watu wangu" BWANA anamfananisha Yeremia na mtu anyepima fedha ili kutambua ni safi kiasi gani. Watu ni kama fedha ambayo Yeremia anaipima na dhambi zao ndiyo uchafu katika zile fedha.

utachunguza

"utagundua"

njia zao

"vitu wanavyofanya."

wanaoenda huko na kule wakiwasingizia wengine

"na daima huwasingizia watu"

Mifuo inafukuta kwa moto unaozunguka; risasi inaunguzwa na moto

virai hivi vinasisitiza kuwa mpimaji anafanya kazi kwa bidii kuipima fedha

Risasi tu ndiyo inyotoka kati yake

"mpimaji anendelea kupima"

kwa sababu uovu haujaondolewa

"kwasababu sehemu mbovu hazijaondolewa"

Wataitwa taka za fedha

"watu wataita 'fedha isiyo na thamani'"

Jeremiah 7

Jeremiah 7:1

Hili ni neno la BWANA lililomjia Yeremia

"Huu ni ujumbe ambao BWANA aliutuma kwa Yeremia

ndilo neno

"ujumbe ambao BWANA yuko tayari kuutoa kwa Yeremia

Simama ukaseme

"BWANA anatoa amri hii kwa Yeremia

kumwabudu BWANA

"kwa sababu ya kumwabudu BWANA"

Jeremiah 7:3

Taarifa kwa ujumla

Huu ndio ujumbe ambao BWANA antaka kumpa Yerermia kwa ajili ya watu wa Yuda.

Tengenezeni njia zenu na kufanya mema

"Ongozeni kwa maisha mema na matendo mema"

muishi hapa

katika nchi ya Israeli. ambayo ina hekalu ambalo ni kitovu chake

msitumainie maneno ya uongo mkisema

"Msitumainie maneno yanuongo kwa kusema"

Hekalu la BWANA! Hekalu la BWANA! hekalu la BWANA!

"Hili ni hekalu la BWANA kwa hiyo kuna uhakika wa kwamba hakuna atakayeliharibu."

Jeremiah 7:5

Taarifa kwa ujumla

Haya ni maneno ya BWANA kwa watu wa Yuda.

kama mtatoa hukumu ya haki kabia

"kama mtafanya kabisa"

kama mtazitengeneza njia zenu na kufanya mema

Tazama 7:3

kama mtatoa hukumu ya haki

"kama mtawatendea watu kwa haki

kama hamtamnyonya ayekaa katika nchi

"kuwatendea vyema wageni wanaokaa katika nchi"''

yatima

watoto ambao baba zao wameshafariki

hamtamwaga damu ya mtu asiye na hatia

"hamtaua watu wasio na hatia."

kama hataenda

"hamtaabudu"

kwa ajili ya maumivu yenu

"ili kwamba vitu vibaya vkataokea kwako"

mahali hapa

katika nchi ya Israeli

nitawaacha mkae

"nitawaacha muishi"

hata milele

"na milele"

Jeremiah 7:8

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kuongea na watu wa Yuda kupitia kwa nabii Yeremia.

Tazama!

Neno "tazama" linaonyesha kuwa maswali yafuatayo yana umuhimu

Mnatumainia maneno ya uongo ambayo hayawasaidii

"Mnadhdani kuwa nitaiokoa Yerusalemu kwa kwa sababu nitlilinda hekalu langu. Lakini huo ni uongo!"

Je, mnau, mnaiba, mnafanya uzinzi?

"Mnaua, mnaiba, mnafanya uzinzi"

Mnaapa kwa uongona kufukiza uvumba kwa Baali na kwenda kwa miungu mingine ambayo hamkuijua?

"Mnadanganya hata katika viapo vyenu na kumwabudu Baali na miungu mingine."

Je, mnakuja na kusimama ... kufanya machukizo yote haya?

"Kisha mnakuja kwenye nyumba yangu na kusema, ''BWANA atatuokoa" ili kwamba ninyi muendelee kufanya dhambi."

Je, hii ndiyo nyumba inyobeba jina langu, pango la wanyang'nyi mbele ya macho yenu?

"Nyumba hii ni pango la wanyang'anyi mbele ya macho yenu!"

wanyang'anyi

"wezi" au "watu wanaoiba vitu toka kwa watu"

BWANA asema

Tazama 1:7

Jeremiah 7:12

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kumwambia Yuda kupitia kupitia kwa nabii Yeremia

kwa hiyo uende

"kwa hiyo ukumbuke" au "tafakari"

kwa hiyo sasa kwa sabasbu ya matendo yako haya yote

"kwa sababu ulikuwa unafanya mambo haya yote"

mara kadhaa

"tena na tena"

Jeremiah 7:16

Usiwaombee watu hawa ... na usinisihi

"usiniombe mimi ukisema niwabariki watu hawa"

usiinue maombolezo ya kilio

"usilie kwa huzuni"

kwa niba yao

"kwa ajili ya faiada yao"

usinisihi

"usiniombe"

ili kunikasirisha

"kunikasirisha"

Jeremiah 7:19

Ni kweli wananikasirisha ... wananikasirisha

"kweli wananisumbua ... wananisumbua"

Ni kweli wananikasirisha mimi?

"Ni kweli hawanisumbui?

Je, si wao wanaojikasirisha? ... ili kwamba aibu iwe juu yao?

"Wanajitaabisha wenyewe kwatabia zao za aibu"

Tazama

Neno hili linavuta usikivu kwa kile kinachofuata. "Sikiliza kwa makini kwa sababu hili ni la muhimu

hasira na ghadhabu zangu zitamwagwa mahali hapa

"Nitawadhibu watu wa mahali hapa."

Hasira na ghadhabu

Maneno haya yana maana moja. Yametumika kusisitiza ukali wa hasira yake

itawaka

kiwakilishi "i" kietumika kuonesha hasira za BWANA."

nayo haitazimishwa

"haitazuiliwa kuwaka" au "sitazuiliwa kuwa na hasira"

Jeremiah 7:21

Jiongezeeni sadaka za kuteketezwa katika dhabihu zenu na nyama zake.

Ingwa BWANA hutaka sadaka, hakutaka tena sadaka zao kwa sababu walibaki kuwa waasi baada ya kutoka hekaluni

Jeremiah 7:24

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kuwakumbusha wa Yuda jinsi watu wa Israeli walivyoasi

kwa kufuata mipango yao ya uasi ya mioyo ya maovu

"kwa kufuata mipango yao kwa sababu walikuwa waovu na wasumbufu

kwa hiyo walirudi nyuma badala ya kuendelea mbele

"kwa hiyo walikataa kunisikiliza mimi, badala ya kunisikiliza kwa makini"

watumishi wangu

"watumishi wangu wote

Niliendelea kuwatuma

"kwa bidii niliwatuma kila siku"

manabii wangu, kwenu

neno "kwenu" linamaanisha watu wa Yuda na mababu zao wote.

Hawakunisikiliza

neno "ha" linamaanisha watu wa Israeli walioishi tangu mababu zao kutoka Misri.

walishupaza shingo zao

"kwa ukatili walikataakunisikiliza"

waikuwa waovu zaidi

"kila kizazi kilikuwa cha uovu"

Jeremiah 7:27

Kwa yatangaze maneno haya ... Tatangaze mabo haya ...

Virai hivi vinamaanisha kitu kimoja. "Waambieni ujumbe wangu lakini hawatanisikiliza na kubadili njia zao mbaya."

sauti ya BWANA

Tazama 3:23

Ukweli umeharibiwa na kukatwa kutoka kwenye vinywa vyao

"watu hongea uongo tu"

Jeremiah 7:29

wana wa Yuda

"kizazi cha Yuda"

amekikataa na kukitupa

manano haya yana maana moja, Yanasisitiza kuwa BWANA hatakuwa na jambo lingine la kufanya kwa watu wa Israeli.

Kuzitupa

"kuziacha pekee yake" au "kupuuzia"

mbele ya macho yangu

"na mimi nikiona" au "katika fikra zangu"

Jeremiah 7:31

Taarifa kwa ujumla

BWANAanaendelea kuelezea maovu ambayo watuwa Yuda wamefanya.

Mahali palipoinuka pa Tofethi

Hili ni neno la mahali ambapo wana wa Israeli walienda kuwatoa sadaka watoto wao kwa miungu ya uongo kwa kuwateketeza kwa moto.

Kwenye bonde la Ben Hinomu

Hili ni jina la binde ambalo liko kusini mwa mji wa Yerusalemu, mahali ambapo watu walitoa sadaka kwa miungu ya uongo.

kwenye moto

"kwenye moto kama sadaka"

katika akili zangu

"na kikuwahi kufikiri hata kuliamuru jambo hili"

kwa hiyo tazama

neno "tazama"linaongeza msisitizo kwa kile kinachofuata."

siku zinakuja

"katika siku za usoni"

asema BWANA

Tazama 1:7

hapataitwa tena

"watu hawatapaita"

bonde la machinjio

"bonde la mauaji"

watazika maiti

"watu wa Yuda watazika wafu"

mpka eneo lote lienee

"hakuna eneo litalobaki"

Jeremiah 7:33

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kuongea

Mizoga

"watu waliokufa"

watu hawa

"watu wa Yuda"

ndege wa angani

Tazama 4:23

wanayama wa duniani

"wanyama wa mwituni"

wa kuwafukuza

"wa kuwatisha ili wakimbie"

Nitazikomesha

"Nitaziondoa kutoka

sauti za kuinuliwa na vicheko

"sauti za watu wanaofurahia"

sauti ya bwana arusi na ya bibi arusi

"watu kuona"

Jeremiah 8

Jeremiah 8:1

Taarifa kwa ujumla

Yeremia amemaliza kuwaambia watu wa Yuda kitakachotokea katika nchi.

Wakati huo

Tazama 7:31, 7:33

asema BWANA

Tazama 1:7

wataleta

neno "wa" linamaanisha watu watakaoiangamiza Yerusalemu.

wakuu wake

"wafalme wa Yuda"

wataitandaza

"neno "wa" linamaanisha mifupa ya watu wa Yuda

hivi vitu katika anga vimenifuata na kunitumikia

"vitu hivi katika anga ambavyo vilinipenda na kunitumikia," kiwakilishi "vi" kinamaanisha watu wa Yuda.

kwamba vimetembea na kutafuta

Tazama 2:23

na kutafuta

"na kwamba wameuliza juu ya"

mifupa haitakusanywa na kuzikwa

"hakuna atakayekusanya mifupa na kuizika."

watakuwa kama mavi

"BWANA anaonesha jinsi ambavyo watakuwa si wa kupendeza."

kama mavi

"kama mbolea"

juuya uso wa dunia

"katika ardhi yote"

ambalo nimewafukuza

kiwakilishi "me" kinawakilisha watu wa Yuda

watachagua mauti badala ya uzima kwa ajili yao, wote ambao watasalia kutokana na taifa hili ovu

"wale ambao bado wamebaki kutoka katika familia hii y a waovu watataka kufa badala ya kuishi"

Jeremiah 8:4

Kwa hiyo uwaambie

BWANA anaongeana Yeremia

uwaambie

"kwa watu wa Yuda"

Je, kuna mtu anayeanguka na hasimami?

"Mnajua kuwa mtu anapoanguka, husimama."

Je, kuna mtu anayepote na hajaribu kurudi?

"mtuu anapopotea, hujaribu kurudi kwenye njia sahihi

Kwa nini hawa watu, Yerusalemu, wamegeukia uasi daima?

"Haiingii akilini kwamba hawa watu wa Yerusalemu wamegeukia uasi daima."

Jeremiah 8:6

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaongea juu ya watu wa Yuda

hawakuongea kilicho sahihi

"hawakusema kilicho sahihi"

uovu wake

"kwa sababu ya uovu wake"

Nimefanya nini

"Nimefanya jambo baya sana"

kila mmoja wao huenda anakotaka

"watu wote wanaendelea kwa bidii kufanya uovu huohuo."

kama farsi aendaye kasi vitani

Watu wanatamani sana kufanya maouvu kama vile farasi hukimbia kwakasi kwenda vitani kwa sababu hutamani kufika kule.

farasi dume

huyu ni farasi dume

Hata koikoi angani hujua wakati sahihi; na njiwa pori, na mbayuwayu, na korongo

Ndege hujua wakati sahihi wakuondoka kwenye nchi ya baridi kwenda kwenye nchi ya joto.

koikoi, njiwa, mbayuwayu na korongo

Hawa ni ndege tofauti ambao hurukka kwenda kwenye maeneo ya joto kabla maeneo yaohayajawa na baridi

huhama kwa wakati sahihi

"huhama kutoka nchi ya baridi kwenda kwenye nchi ya joto"

Jeremiah 8:8

Taarifa kwa ujumla

Haya ni maneno ya BWANA kwa watu wa Yuda.

Kwa nini mnasema, "sisi tuna hekima! na sheria ya BWANA tunayo?"

"Msisema kuwa mna hekima, na sheria ya BWANA mnayo."

Kwa nini mnasema

kiwakilishi cha "mna" kinawakilisha watu wa Yuda.

Kalamu yenye uongo ya mwandishi imefanya uongo

"Mambo ya uongo ambaYo walimu wa sheria wamekuwa wakiandika yamewapeni mawazo ya uongo juu ya sheria za BWANA "

Wenye hekima wataabishwa

"Hawa watu wanofikiri kuwa wanahekima watajisikia kuaibika"

Wameyeyuka na kunaswa

"Aduii watawateka na kuwachukua"

hekima yao ni kwa ajili ya matumizi gani?

"kwa hiyo hicho kinachoitwa hekima hakina kazi yeyote njema kwao"

kwa wale watakaowamiliki

"watu watakaoitawala nchi yao"

kwakuwa kuanzia kijana ... wote wanasema uongo

Tazama 6:13

Jeremiah 8:11

Taarifa kwa ujumla

Haya ni maneno ya BWANA kwa watu wa Yuda

Kwa kuwa wameitibu jeraha ya binti za watu wangu ... asema BWANA

Tazama 6:13

jani litanyauka

"jani litakauka"

na chote nilichowapatia kitaisha

Hi inaweza kumaanisha 1) "Niliwapa maelekezo watu wangu, lakini watu wangu hawakutii hayo maelekezo. 2) "kwa hiyo, nimewatoa hawa watu kwa adui zao, ili adui zao wawakanyage."

Jeremiah 8:14

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea na ujumbe wake kwa kutuambia kile watu wa Yuda watakachosema wakati huo wa adhabu.

Kwa nini tunakaa hapa

"Hatupswi kukaa hapa."

Njono pamoja; twendeni kwenye hiyo miji yenye maboma

Tazama 4:4

miji yenye maboma

"miji yenye kuta imara na askari wa kuilinda

na tutakaakimya kule katika kifo

"nasi tutafia huko"

BWANA Mungu wetu atatunyamazisha

"kwa sababu BWANA Mungu wetu atatuua"

Atatufanya tunywe sumu

"Ataufanya tunywe sumu" inamaanisha hukumu ya Mungu.

lakini tazama, kutakuwa na

"lakini eleweni, kutakuwana"

lakini hakutakuwa na jema

"lakini hakna jema litakalotokea"

Jeremiah 8:16

Taarifa kwa ujumla

BWANA anendeleza ujumbe wake juu ya adhabu inayokuja kwa watu wa Yuda

Mkoromo wa farasi wake umesikika kutoka Dani

"Watu wa Dani wanaiasikia sauti ya jeshi la adui likija kuivamia Yuda,"

farasi

farasi dume

Dunia nzima inatikisika

"watu wa nchi wanatikisika kwa hofu"

kwa sababu ya sauti ya kukaribia kwa farasi wake wenye nguvu

"watakaposikia sauti ya farasi mwenye nguvu wa adaui"

sauti ya farasi

sauti ambayo farasi huitoa

kwa kuwa watakuja

Kiwakilishi "wa" kinmaanisha jeshi linalovamia

kuiangamiza nchi

"na kuiharibu nchi."

Ninawatuma nyoka kati yenu

"Ninawatuma askari wa adui ili kuwapigeni ninyi."

fira ambao hawawezi kuzuiliwa kwa uganga

Fira ambao huwezi kuwafukuza kwa uchawi

watawauma

"watawashambulia" au "watawaangamiza"

asema BWANA

Tazama1:7

Jeremiah 8:18

Taarifa kwa ujumla

Yeremia na BWANA wana mazungumzo juu ya watu wa Yuda.

Huzuni yangu haina ukomo, na moyo wangu unaugaua

Aya hii kwa Kihebrania inatafsiriwa tofauti sana leo.

Huzuni yangu haina ukomo

kiwakilishi "yangu" kinamwakilisha Yeremia. "Nina huzuni sana"

na moyo wangu unaugua

kiwakilishi cha "wangu" kinamwakilisha Yeremia. "Ninajihisi kuugua ndani yangu."

Sikia sauti ya mauivu ya binti wa watu wangu kutoka mbali!

Hii inaweza kumaanisha1) "watu wa Yudsa wanaita wakiwa utumwani mbali sana 2)"Watu wa Yuda wanaita kutoka katika nchi ya Israeli yote."

binti wa watu wangu

Israeli ni kama binti

Je, BWANA hayumo sayuni?

Yerusalemu inaitwa Sayuni pia

Je, BWANA hayumo Sayuni? Mfalme wake hayumo ndani yake?

"Kwa nini BWANA hatuokoi kama ndiye mfalme wa Yerusalemu?

Kwa nini sasa wananichukiza kwa vitu vya kuchongwa na sanamu za kigeni zilizo batili?

"Kama wanataka niwaokoe, basi wasinichukize kwa kuabudu sananmu zao."

Jeremiah 8:20

Taarifa kwa ujumla

Yeremia anaendelea kuongea juu ya watu wa Yuda

Mavuno yamepita

"wakati wa mavuno umeisha

Lakini sisi hatujaokoka

"Lakini BWANA hajatuokoa,"

Nimeumia kwa sababu ya binti wa watu wangu

"Ninajisikia vibaya kwa sabau watu wa Yuda wanapitia mambo mabaya sana."

Je, kule Gileadi hakuna dawa? Je, huko hayuko mponyaji?

"Kuna dawa Gileadi! Kuna daktari Gileadi!"

Kwa nini uponyaji wa binti wa watu wangu hauatokei?

"Lakini watu wangu wana vidonda vya kirohokiasi kwamba hiyo dawa na hao waganga hawaezi kuviponya."

Jeremiah 9

Jeremiah 9:1

Taarifa kwa ujumla

BWANA na Yeremia wanaendelea kuongea juu ya watu wa Yuda

Kama kichwa changu kingetoa maji, na macho yangu kuwa chemichemi ya machozi

"Natamani kama ningetengeneza machozi zaidi!"

usiku na mchana

"muda wote."

binti wa watu wangu

Tazama 4:11

ambao wameuawa

"ambao adui amewaua."

Kama mtu angenipatia

"Natamani kama mtu angnipatia"

mahali pa wasafari nyikani nikae

Hii inamaanisha jengo la watu wanaosafairi nyikani, amabalo wanaweza kutulia na kulala wakati wa Usiku.

kuwatelekeza watu wangu

"kuwaacha watu wangu"

kundi la webye hiana

"kundi la watu wanaoweza kusaliti watu

asema BWANA

Tazama 1:7

Huupinda ulmi wao kana kwamba ni upinde ili wapate kuongea uongo

Kuongea uongo hufanywa na ndimi za waovu.

lakini si kwa uaminifu wao

"si waaminifu kwa BWANA."

si kwa uaminifu wao

"hawana nguvu katika kweli."

wanatoka uovu mmoja hadi mwingine

"wanaaendelea kufanya mambo maovu."

Jeremiah 9:4

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kuongea na Yeremia juu ya watu wa Yuda.

Kila mmoja wenu

neno "wenu" linawawakilisha watu wa Yuda

awe mlinzi wa jirani yake na usimwamini hata ndugu yako yeyote

"uwemwangalifu kwa kutowaamini ndugu zako Waisraeli, na usimwamini hata ndugu yako"

kila jirani anatembea akilaghai

Tabia ya kuongea uongo juu ya kila mmoja ni ulagahai.

Kila mwanamuume anamkejeli jirani yake na haongei ukweli

"Watu wote wanakejeliana na hawasemei ukweli"

Ndimi zao hufundisha vitu vya uongo

"wanafundisha vitu ambavyo si vya ukweli."

Hujidhofisha ili kusema uongo

"wamechoka kwa sababu ya kutenda maovu mengi"

makazi yenu yako kati ya udanganyifu

kuishi na miongoni mwa waongo ni sawa na kuishi katikati ya uongo.

kwa uongo wao wanakataa kunitambua mimi

"Kwa kusema uongo huu wote, watu wa Yuda wameshindwa kunitii mimi kama Mungu."

asema BWANA

Tazama 1:7

Jeremiah 9:7

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kuongea juu ya watu wa Yuda.

binti wa watu wangu

Tazama 4:11

Ndimi zao ni mishale iliyochongoka

Ndimi huumiza watu kwa uongo katika njia sawa na mishale iliyochongoka inavyoumiza

Kwa midomo yao wanatangaza amani pamoja na jirani zao

"Wanasema kwa maneno yao kuwa wanataka amani na majirani zao."

lakini katika mioyo yao wanadanganya wakati wa kusubiri

"lakini katika uhalisia wanataka kuwaangamiza jirani zao."

Kwa nini nisiwaadhibu kwa sababu ya mambo haya ... kwa nini nisijilipizie kisasi kwa taifa ambalo liko kama hili?

Tazama 5:7

Jeremiah 9:10

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kuongea juu ya watu wa Yuda. Katika mstari wa 12, Yeremia anatoa maoni yake.

Nitaimba wimbo ...kwa ajili ya milima

BWANA anaomboleza kwa ajili ya nchi ya Israeli kana kwamba mtu amekufa.

milima

mahali ambapo wanyama hupata malisho

kwa kuwa wameteketezwa

"kwa kuwa kuna mtu ambaye ameyateketeza hayo malisho

Hawatasikia sauti ya ngombe yeyote

"Hakuna ambaye atasikia sauti ya ng'ombe

maficho ya mbweha

"mahali ambapo mbweha hujificha"

mbweha

mbwa wakali

isiyokaliwa na watu

"mahali ambapo watu hawakai

Ni nani mwenye hekima anayeyaelewa haya

"kama manabii wenu ni wenye hekima kweli, wanapaswa kuelewa kwa nini nchi imeharibiwa

Je, kinywa cha BWANA kinatanga nini kwake ili awaeze kuyasema

"Kama kweli BWANA anasema na manabii wenu, basi wanapaswa kuwaambia kile ambacho BWANA anasema juu ya uharibifu wa nchi."

kwa nini nchi imepotea

"Lakini manabii wenu hawana hekima na BWANA hasemi nao, kwa hio hawajui kwa nini nchi imeharibika"

Jeremiah 9:13

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kuonge juu ya watu wa Yuda

Ni kwa sababu wameziacha

"Nchi imeharibiwa kwa sabasbu watu wa Yuda hawakutii"

hawaisikilizi sauti yangu

""hawatilii maanani kwa vitu ambavyo ninawaambia."

kwa kuifuata

"au kuishi kwa namna ambayo nawataka waishi"

wameishi kwa ushupavu wa mioyo yao

"wamekuwa wasumbufu na wameishi kwa jinsi wanavyotaka kuishi"

na wamewafuata Mabaali

"na wameabudu miungu ya uongo"

Jeremiah 9:15

Taarifa kwa ujumla

BWANA anaendelea kuongea juu ya watu wa Yuda.

pakanga

"mmea ulio na radha chungu"

Ndipo nitakapowasambaza kati ya mataifa

"Kisha nitawalzimisha kuondoka hapa na kuishi katika nchi nyingi"

Nitatuma upanga kwa ajiliyao

"Nitatuma jeshi la askari kuwapiga."

Jeremiah 9:17

Taarifa kwa ujumla

BWANA anawaambia watu wa Yuda kuomboleza kwa ajili ya uharibifu wa nchi ujao.

Waiteni waliaji; waje. Tumeni wanawake wenye taaluma ya kuomboleza juu yetu, waje.

"Tafuteni wanawake waliofunzwa kuomboleza na muwaleta wanawake hao hapa."

Waiteni waliaji

"Waiteni wanawake wenye taaluma ya kulia"

waje

"waambieni wanawake waje"

Tumeni wanawake wenye taaluma ya kuomboleza

"Temeni watu waende kuwatafuta wanawake wenye taaluma ya kuomboleza."

Waje haraka waimbe wimbo wa maombolezo juu yetu.

"waambieni wanawake waje haraka na waimbe wimbo wa kuomboleza kwa ajili yetu"

ili kope zetu zitokwe na machozi na macho yetu yabubujikwe na maji

"ili kwamba tulie kwa bidii"

Jeremiah 9:19

Taarifa kwa ujumla

Haya ni maneno ya BWANA juu ya watu wa Yuda

Kwa kuwa sauti ya kilio imesikika Sayuni

"Watu wanalia kwa sauti Yerusalemu"

Jinsi tulivyoharibiwa

"Tunasikitika sana"

Tumeaibishwa sana, kwa kuwa tumeitelekeza nchi tangu walipoangusha nyumba zetu

"aibu yetu ni kubwa, kwa sababu adui wameharibu nyumba zetu, na tulipaswa kuiacha nchi ya Israeli"

sikieni neno la BWANA zingatieni ujumbe unaokuja toka kinywani mwake.

Sentensi hizi mbili zinasisitiza amri ya kusikiliza kile ambacho BWANA anasema.

Kisha wafundisheni binti zenu wimbo wa maombolezo, na kila mwanamke wa jirani wimbo wa kilio.

Kisha wafundisheni watu wengine jinsi ya kuomboleza."

Jeremiah 9:21

Taarifa kwa ujumla

Haya ni maneno ya BWANA juu ya nyumba ya Yuda.

Kwa kuwa vifo vimekuja kupitia dirishani

BWANA anasema kuwa BWANA atakapowaangamiza watu wa Israeli watalinganisha kifo na mtu anayeingia kuptia dirishani kwa lengo la kuangamiza watu waliojificha ndani yake

mahali petu

Nyumba zenye maboma ambapo wafalme huishi. Kifo kinachokuja kwa tajiri na masikini kinafanana.

vinaharibu watoto kutoka nje

"Kifo kinaua watoto mitaani."

na vijana kweye viwanja vya mji

"na kifo kinaua vijana kwenye viwanja vya mjij."

viwanja vya mji

"maeneo ya maasoko"

asema BWANA

Tazama 1:7

mizoga ya wanaume itaanguka mavi kwenye mashamba, na kama mabua baadaya mvunaji

"maiti zitatapakaa maeneo yote."

na kama mabua baada ya mvunaji

"na kama mabua yaangukapo kila mahali baada ya mkulima kuyakata."

na hapakuwa namtu wa kuyakusanya

"na hapatakuwa namtu wa kukusanya maiti"

Jeremiah 9:23

Taarifa kwa ujumla

Haya ni maneno ya BWANA

Usimwache mtu mwenye busara ajivuna kwa ajili ya hekima yake

"Mtu mwenye busara asijivune kwa sababu yeye ni mwenye hekima"

Usimwache mtu tajiri ajivunie utajiri wake

"Mtu tajiri asijivune kwa sababu ni tajiri"

acha iwe hivi, yeye awe na busara na kunijua mimi

"kwamba anajua kuwa mimi ni nani na kuishi katika njia ambazo zinanipendeza mimi"

Kwa kuwa momi ni BWANA

"Kwa sababu watu wanapaswa kujua kuwa mimi ni BWANA"

Ni katika hili kwamba ninafurahia

"Na inanifurahisha mimi watu wanapoishi kwa uaminifu katika agano, kwa haki na katika hukumu za haki

asema BWANA

Tazama1:7

Jeremiah 9:25

Taarifa kwa ujumla

Haya ni maneno ya BWANA

siku zinakuja

"kutatokea wakati"

asema BWANA

Tazama 1:7

nitakapowaadhibu wote ambao hawajatahiriwa ambao wako hivyo hivyo katika miili yao

Hii inamaanisha watu wa Israeli ambao wameingia katika agano la BWANA kwa kutahiriwa ki mwili, lakini hawakufuata sheria zake.

Na watu wote wanaonyoa denge

Hii inawezekana kumaanisha wale watu wanaokata nywele zao kuwa fupi kwa lengo la kuabudu miungu ya kipagani.

Kwani mataifa yote haya hayajatahiriwa

"Kwa sababu mataifa yote haya hayajaingia kwenye agano na BWANA kwa njia ya tohara."

na nyumba yote ya Israeli ina moyo ambao haujtahiriwa.

"na nyumba yote ya Israeli hawajalinda agano LA BWANA kwa kumtii."

Jeremiah 10

Jeremiah 10:1

Taarifa kwa ujumla

BWANA amemaliza kuwakumbusha watu wa Yuda, pamoja na Misri, Edomu, Amoni, Moabu, na watu wote ambao wataadhibiwa

msijifunze njia za mataifa

"Msifuate imani ya mataifa ya Kipagani "

msishangazwe

"kuwa na mashaka" au "kuogopa"

na ishara za mbinguni

"kwa vitu vigeni angani"

kwa kuwa mataifa hushangazwa na haya

"kwa kuwa watu wa mataifa huogopa vitu vigeni wanavyoviona angani"

Jeremiah 10:3

Taarifa kwa ujumla

BWANA amemaliza kuwakumbusha kuwa wasijifunze njia za matiafa wala kutishwa na vitu wanavyoviona angani.

fundi

"mtu mwenye ujuzi wa kazi za mikono"

sanamu za kutisha ndege

Hii ni sanamu yenye sura ya mtu iliyotengenezsa ili kutisha ndege ili kuzuiza kula mazo

matango

Ni ainaya mboga za majani ambayo huwa na umbo refu, na rangi ya kijani na nofu nyeupe nayo huwa na maji mengi.

Jeremiah 10:6

Taarifa kwa ujumla

Yeremia alikuwa akiongelea ibaada za sanamu

Ni nani asiyekuwa na hofu juu yako, mfalme wa mataifa?

"Kila mmoja lazima akuogope, mfalme wa mataifa"

ndicho unachostahili

"kile ulichovunva"

Jeremiah 10:8

wote wako sawa, ni kama wanayama na wapumbavu

"kila mmoja wao ni mpumbavu"

wanafunzi wa sanamu ambazo si chochote isipokuwa miti tu

"wanajaribu kujifunza toka kwa sanamu ambayo ni kipande cha mti"

sonara

"mtu mwenye ujuzi wa kazi za mikono"

Tarshishi ... ufazi

Ni maeneo ambayo dhahabu na fedha zinapatikana

dhahabu kutoka Ufazi ilyotengenezwa na sonara,ni kazi ya ustadi

"dhahabu kutoka Ufazi amabyo sonara mwenye ujuzi ameitengeneza"

mavazi yao ni rangi y samawi na urujuani

"watu waliivalisha sanamu kwa mavazi mazuri

matetemeko

"mtikisiko"

Jeremiah 10:11

Taarifa kwa ujumla

Mungu anamwambia Yeremia

Aliyeiumba dunia kwa nguvu zake ... kwa fahamu zake

"Muumbaji yuko imara na mwenye hekima. Alitengeneza dunia na anga."

Sauti yake ndiyoitengenezayo muungurumo wa maji

"Yeye hutawala dhoruba angani kwa kuongea"

naye huzileta mbingu katika mwisho wa dunia

"Hutengeneza mawingu dunianikote"

hazuna yake

ni jengo ambalo vitu hutunzwa

Jeremiah 10:14

amekuwa mjinga

"anapungukiwa maarifa" au "hajui"

Fungu la Yakobo

"ambaye watu wa Israeli humwabudu"

yeye ndiye aliyeviumba

"muumbaji wa vitu vyote" au "ambaye aliumba vitu vyote"

Jeremiah 10:17

Kusanya vitu vyako

"Kusanya mali zako"

Tazama

neno "tazama" limetumika kusisitiza yale yanayofuata

Ni tayari kuwatupa wakazi wa nchi nje wakati huu

"Nitawafanya watu wanaoishi kwenye nchi kuiacha nchi"

wakazi wa nchi

"watu wanaoishi katika nchi"

huzuni

"maumivumakubwa"

Jeremiah 10:19

Taarifa kwa ujumla

Yeremia anaongea kana kwamba yeye ndiye kabila yote ya Israeli.

Ole wangu! kwa sababu ya mifupa yangu iliyovunjia, jeraha zangu zimeumia

"Tuko katika huzuni kubwa kama mtu ambaye mifupa yake imevunjika na kuumia"

Hema yangu imeharibiwa, na kamba za hema yangu zote zimekatwa.

"adaui ameuharibu mji kabisa"

Wamewachukua

"adaui wamechukua"

Hakuna tena mtu wa kuitandaza hema yangu au wa kuziinua pazia za hema yangu

"Hakuna mtu wa kuujenga tena mji wetu"

Jeremiah 10:21

wamesambaa

"wametenganishwa na kuwa na uelekeo tofauti

mbweha

mbwa waakli wa mwitu wanaopatikana Afrika

Jeremiah 10:23

Mwaga hasira zako kwa mataifa

"Waadhibu vikali watu wa mataifa"

wamemla Yakobo na kumwangamiza kabisa na kuyafanya makao yake kuwa ukiwa

Neno "kumla" na "kumwangamiza" yanamaanisha kitu kilekile yanayomaanisha "kumwangamiza kabisa" Tametumika kuonesha uharibifumkubwa kwa Israeli.

kuyafanya makao yake kuwa ukiwa

"kuharibu nchi ambayo hukaa"

Jeremiah 11

Jeremiah 11:1

wenyeji wa Yerusalemu.

"watu wanaoishi Yerusalemu"

Jeremiah 11:3

tanuru

inapokanzwa chuma kwa fomu ya maji

nchi iliyojaa maziwa na asali

Hii inamaanisha kwamba ardhi itakuwa tajiri na yenye mazao, kwa hiyo kutakuwa na chakula cha kutosha kwa kila mtu. AT "ardhi ambayo ni bora kwa ng'ombe na kilimo"

Jeremiah 11:6

nzuri

"mbaya"

Kila mtu amekuwa akitembea katika ukaidi wa moyo wake mbaya.

"Kila mtu amekataa kubadili na kuendelea kufanya mambo mabaya ambayo wanataka kufanya"

Jeremiah 11:9

njama

mpango wa siri wa kufanya kitu ambacho ni hatari au kinyume cha sheria

wenyeji wa Yerusalemu

"watu wanaoishi Yerusalemu"

Jeremiah 11:11

Tazama

"Kusikiliza" au "Jihadharini na kile ninachokuambia"

Jeremiah 11:14

Kwa hiyo wewe ... kwa niaba yao

Tafsiri hii kwa njia ile ile uliyetafsiriwa "Na wewe ... kwa niaba yao" katika 7:16.

Lazima usiomboleze

"Usifanye kilio kikubwa cha huzuni"

Mpendwa wangu anafanya nini nyumbani kwangu?

Swali hili linaweza kufanywa kama taarifa ya kukemea. "Mpendwa wangu, ambaye amekuwa na nia mbaya sana, haipaswi kuwa nyumbani kwangu."

Mpendwa wangu anafanya nini nyumbani kwangu?

Kifungu hiki kwa Kiebrania ni ngumu sana, na matoleo mengi yanatafsiri kwa njia tofauti.

nyumba

hekaru

mpendwa wangu

Watu wa Israeli wanazungumzwa kama kwamba walikuwa mwanamke mmoja aliyependwa sana.

Katika siku za nyuma Bwana alikuita mti wa mzeituni wenye majani

Katika Agano la Kale, watu mara nyingi walitamka kama miti au mimea

atawasha moto juu yake

Maneno haya yanaendelea mfano wa mti. Moto unasimamia kama uharibifu wa watu.

Jeremiah 11:17

yeye aliyekupanda

"aliyekuweka wewe kuishi katika nchi ya Israeli na Yuda"

Jeremiah 11:18

unayeongozwa na mchinjaji

"kwamba adui zangu walikuwa wakiongoza kwa mchinjaji"

ili jina lake lisikumbukwe tena

"Watu hawatakumbuka tena jina lake"

Jeremiah 11:21

Anathothi

mji maalum kwa ajili ya makuhani kuishi

Vijana wao wenye nguvu

wanaume wakati wa nguvu zaidi ya maisha yao

Hakuna hata mmoja atakayeachwa

"Sitawaacha hata mmoja wao"

Jeremiah 12

Jeremiah 12:1

Taarifa za jumla

Yeremia anaongea na Bwana.

mbali na mioyo yao

hawakukupendi au kukuheshimu wewe

Jeremiah 12:3

Taarifa za jumla

Yeremia anaendelea kusema na Bwana.

Waondoe kama kondoo wa kuchinjwa

"Tayari kuwaadhibu watu waovu"

Je! Nchi itakauka kwa muda gani.....sababu ya uovu wa wenyeji wake?

"Rasimu ya sababu kwa uovu wa watu imechukua muda mrefu sana."

Wanyama pori na ndege wamekufa kutoka ukame.

Wanyama na ndege wameondolewa

kuota

"kausha"

Jeremiah 12:5

unawezaje kushindana dhidi ya farasi?....utafanyaje katika misitu karibu na Yordani?

Maswali haya mawili yanalenga kutoa taarifa. AT "huwezi kushindana vizuri dhidi ya farasi ... utashindwa katika misitu karibu na Yordani."

Ikiwa unashuka chini ya nchi iliyo salama

Baadhi ya matoleo ya kisasa yanatafsiri kifungu hiki kwa Kiebrania kama 'Ikiwa unajisikia salama katika nchi ya salama.'

nchi iliyo salama

Hii inahusu nchi ya wazi, ambapo ni rahisi kusafiri haraka, kinyume na vichaka vilivyomo karibu na Mto Yordani, ambako ni vigumu kuhamia.

misitu

vichaka vingi au miti midogo inakua karibu

Jeremiah 12:7

Nimeiacha nyumba yangu; Nimeacha urithi wangu. Nimewatia watu wangu wapendwa mikononi mwa adui zake.

Sentensi hizi tatu zina maana sawa. Kwanza na ya pili huimarisha mawazo ya tatu. (Angalia "Ulinganifu) "Nimewaacha adui za watu wangu kuwashinda."

hiena

aina ya mbwa kutoka Asia na Afrika ambayo inakula mwili wa wanyama waliokufa

ndege wa mawindo

ndege ambazo wanashambulia na kula wanyama

Jeremiah 12:10

Wamevunja juu ya

'"wamevunja chini ya miguu yao" au "wameharibu"

sehemu yangu ardhi

"ardhi niliipanda"

Wamemfanya

Neno "yake" linamaanisha Nchi ya Ahadi

yeye ni ukiwa

Neno "yeye" linamaanisha Nchi ya Ahadi

haya moyoni mwake

"kujali" au "kulipa kipaumbele"

Jeremiah 12:12

wazi

"sio kufunikwa" au "tupu"

Upanga wa Bwana unakula

Bwana anatumia majeshi haya kuwaadhibu watu wake

upande mmoja wa nchi hadi mwingine

Hii inahusu nchi yote ya Ahadi

Wana

"Watu wangu wana"

miiba

mimea mikubwa ambayo inafunikwa kwa pointi kali

wamechoka

"huvaliwa" au "amechoka"

Jeremiah 12:14

wanaopiga

kushambulia na kukamata

aliwafanya watu wangu wa Israeli wamiliki

"aliwapa watu wangu Israeli kama warithi"

kuamgamiza

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 1 9.

nami nitainua nyumba ya Yuda kutoka kati yao

kuruhusu watu wa Yuda kuondoka nchi zao za adui na kurudi kwa Yuda

futa

au "kupoteza"

Ninataangamiza mataifa hayo

"nawafanya mataifa hayo kutoka nchi zao na kuhamia maeneo tofauti"

Jeremiah 12:16

Taarifa za jumla

Neno la Mungu kuhusu majirani ya Yuda.

Kisha itakuwa ikiwa.... Baali, basi wao

"Hiyo ndiyo itafanyika ... Baali wao" au "Ikiwa ... Baali, basi hii ndiyo itafanyika"

katikati

katikati

basi watajengwa katikati ya watu wangu

"Nitawafanya kuwa tajiri na wataishi kati ya watu wangu"

nitaling'oa taifa hilo. Kwa hakika litang'olewa na kuharibiwa

"Mimi hakika na kabisa kuondolewa na kuharibu taifa hilo"

hili ndilo tamko la Bwana

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 1:7.

Jeremiah 13

Jeremiah 13:1

kitani

aina ya nguo nzuri sana

nguo

nguo ambazo watu huvaa chini ya nguo zao; chupi

kiuno

sehemu ya kati ya mwili, kwa kawaida nyembamba, kati ya mapaja na kifua

neno la Bwana lilifika kwa

Tazama jinsi ilivyotafasiri hii katika 1:1.

mwamba wa jabali

nafasi kati ya miamba au ufa katika mwamba, kubwa ya kutosha kuweka kitu ndani yake

Jeremiah 13:5

Je! Ubora wa nguo ulikuwa nini wakati Yeremia alipokwenda kutoa mahali alipoficha?

Haikuwa nzuri kabisa.

Jeremiah 13:8

neno la Bwana lilifika

Tazama jinsi ilivyotafasiri hii katika 1:1.

kiburi

"kiburi"

wa Yuda na Yerusalemu

"watu wa Yuda na Yerusalemu"

mbao huenda katika ugumu wa mioyo yao

"ambao wanaendeleza ukaidi"

nyumba zote za

"watu wote wa"

fungwa kwangu

'kukaa karibu na mimi'

hili ndilo tamko la Bwana

Angalia jinsi ilivyotafasiri hii katika 1:7.

Jeremiah 13:12

kujaza ulevi kila mwenyeji wa nchi hii

"kwa sababu watu wote wa nchi hii kunywa"

wafalme wanaokaa kiti cha Daudi

"wafalme wa taifa la Yuda"

gonganisha kila mtu na mwenzake baba na watoto wao pamoja

"kila mtu atapigana na mwingine; hata wazazi na watoto watapigana dhidi ya kila mmoja"

Sitakuwa na huruma

"Siwezi kusikia samahani kwa"

sitawarehemu kutoka kwenye uharibifu

"hautazuia adhabu" au "itawawezesha kuangamizwa" au "itawawezesha kukabiliana na uharibifu"

Jeremiah 13:15

Msiwe na kiburi

"Usihisi kuwa wewe ni bora, mwenye busara, au muhimu zaidi kuliko wengine"

huleta giza

"husababisha giza kuja" Giza linaashiria shida kubwa na kukata tamaa. "Yeye huleta shida kubwa"

kabla ya kuifanya miguu yako kuwa na mashaka

"kabla ya kukusababisha mguu wako juu ya kitu fulani huku ukitembea au kukimbia ili uweke"

ataigeuza sehemu kuwa giza nene

"atasababisha sehemu hiyo kuwa nyeusi kabisa" AT "atakufanya uvunjike moyo"

Jeremiah 13:18

Taarifa za jumla

Bwana anaendelea kuzungumza na Yeremia. Anamwambia Yeremia nini cha kumwambia mfalme wa Yuda na mama wa mfalme

kwa maana taji juu ya kichwa chako, kiburi chako na utukufu wako, umeanguka

"Huwezi tena kuwa mfalme na mama wa malkia" (Angalia hatua ya mfano)

mama wa malkia,

mama wa mfalme.

Miji ya Negebu itafungwa

"Adui zako watafunga miji ya Negebu juu"

Yuda watachukuliwa mateka

"Maadui watachukua Yuda mateka"

Jeremiah 13:20

Taarifa za jumla

Bwana anaongea na watu wa Yerusalemu.

Inua macho yako

"kuelewa nini kitakachotendeka kwako"

Je, ni kundi gani alilokupa, kundi ambalo lilikuwa zuri sana kwako?

"Watu wote wameondolewa."

Je, unasema nini wakati Mungu anawaweka wale ambao uliwafundisha kuwa marafiki?

"Watu ambao ulifikiri walikuwa marafiki wako watawashinda na kutawala juu yenu."

Je, huu si mwanzo wa maumivu ya utungu ambayo yatakuchukua kama mwanamke aliye katika kuzaa?

Bwana anawaambia kwamba kukamata yao ni mwanzo wa maumivu watakayopitia.

Jeremiah 13:22

Taarifa za jumla

Bwana anaendelea kuzungumza na Yeremia. Anamwambia Yeremia nini cha kumwambia mfalme wa Yuda na mama wa mfalme

sketi imefunuliwa

"askari wa majeshi ya kuivamia watainua sketi za wanawake wako". Nguo za wanawake wa Yudea zitavunjwa ili askari wa Babeli waweze kuwashika na kulala nao.

e, watu wa Kushi hubadilisha rangi yao ya ngozi

"Watu wa Kushi hawawezi kubadili rangi yao ya ngozi"

chui hubadilisha madoa yake

"Chui hawezi kubadilisha matangazo yake"

Ikiwa ndivyo, basi wewe mwenyewe, ingawa unazoea uovu, utaweza kufanya mema.

"Huwezi kufanya mema kwa sababu ya uovu wako."

nitawaangamiza kama makapi ambayo yanaangamia katika upepo wa jangwa.

Bwana anasema atawaangamiza watu Wake duniani kote.

Jeremiah 13:25

Hii ndiyo niliyokupa, sehemu ambayo nimekuagiza kwako

"Hivi ndivyo ninavyokufanya kutokea kwako"

hili ndilo tamko la Bwana

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 1:7.

imi mwenyewe nitaondoa nguo zako, na sehemu zako za siri zitaonekana.

"Nitafunua uovu wako."

ubembe

Hii ni sauti ya farasi wa kiume anayetaka farasi wa kike. AT "tamaa."

Je! Hili litaendelea kwa muda gani

Je, itakuwa muda gani kabla ya kusafisha tena

Jeremiah 14

Jeremiah 14:1

Taarifa ya jumla

Bwana, kupitia nabii Yeremia, anazungumzia kuhusu uzinzi wa watu.

neno la Bwana lililomjia

"ujumbe ambao Mungu alizungumza na" Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 1:1.

kuanguka mbali

"kuanguka vipande vipande"

Kilio chao kwa Yerusalemu kimepaa juu

"Wanatoa wito kwa sauti kubwa kwa ajili ya Yerusalemu"

Jeremiah 14:4

Taarifa ya jumla

Bwana, kupitia nabii Yeremia, anazungumzia kuhusu uzinzi wa watu.

Kunguru huwaacha wanawe wake katika mashamba na kuachakuwaacha

"Kunguru huwaacha wanawe wake katika shamba"

mbweha

mkali, mbwa mwitu

Jeremiah 14:7

Taarifa ya jumla

Bwana, kupitia nabii Yeremia, anazungumzia kuhusu uzinzi wa watu.

kwa ajili ya jina lako

"ili kila mtu aweze kuona kwamba wewe ni mzuri sana na unaweka ahadi zako."

tumaini la Israeli

Hii ni jina jingine kwa Bwana.

yeye anayemwokoa

"mwokozi" au "yule anayemwokoa"

kwa nini utakuwa kama ... kama shujaa ambaye hawezi kuokoa mtu yeyote?

Neno "kama" hapa linamaanisha "sawa na."

aliyechanganyikiwa

hawawezi kuelewa au kufikiri wazi

Jeremiah 14:10

Taarifa za Jumla

Yeremia amekuwa akisali na kumwomba Bwana asiwaache peke yao

wanapenda kutanga tanga

"wanapenda kutenda kwa njia iliyo kinyume na mapenzi ya Mungu"

kukumbuka

"anakumbuka" au "anakumbuka"

kwa niaba ya

"kusaidia" au "kusaidia"

kulia

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 14:1

Jeremiah 14:13

Taarifa za Jumla

Bwana amemwambia Yeremia sio kuwaombea watu wa Yuda.

Huwezi kuona upanga

Hapa "upanga" unasimama vita, na "kuona" inamaanisha "uzoefu" au "kuteseka." "Huwezi kupata vita yoyote"

ulinzi

Kuishi katika ustawi na kutokuwepo kwa adui wenye kutishia husemwa kama kama kitu ambacho mtu anaweza kumpa mtu mwingine.

wanatabiri uongo

Ubora unaothibitisha unabii wa uwongo unasemwa kama kama yenyewe unabii. AT "kutabiri kwa udanganyifu"

sikuweza kuwafukuza

Watafsiri wanaweza kuamua kuingiza marudio yasiyo na uhakika na madhumuni ya hatua hii. AT "Sikuwapeleka kutabiri kwa watu wengine"

maono ya udanganyifu na ubatili, uongo unaotokana na mawazo yao wenyewe

Hapa maono na uchawi vinasemwa kama kwamba walikuwa vitu ambavyo vinaweza kwenda kutoka sehemu moja hadi nyingine. Katika 'maono ya udanganyifu na ya maana, uongo wa uongo ambao manabii hao wenyewe wamefikiri'

maono.......uvumbuzi

Maneno haya yanasimama kwa vitendo ambavyo vinasemwa kama ni vitu.

mawazo yao wenyewe

Hapa mawazo yanasemwa kama kwamba walikuwa mahali badala ya uwezo wa kufikiria mawazo.

Jeremiah 14:15

Taarifa za jumla

Yeremia amekwisha kuzungumza na Bwana juu ya mambo ambayo manabii wa uongo wamekuwa wanatabiri

wanatabiri kwa jina langu

Hapa "jina" linawakilisha mawazo ya mamlaka. AT "kutabiri wakati wa kudai mamlaka yangu ya kufanya hivyo"

hakutakuwa na upanga

Hapa "upanga" unamaanisha wazo la vita. AT "hakutakuwa na vita"

nitamwaga uovu wao wenyewe juu yao

Tabia za uadili kama vile uovu mara nyingi huzungumzwa kwa Kiebrania kama kwamba walikuwa maji. Pia, ubora wa uovu umesimama hapa kwa adhabu inayostahiliwa na watu waovu. AT "Nitawaadhibu njia ambayo inastahili kuadhibiwa".

Jeremiah 14:17

kubwa lisilotibika

kukata au kuchumbuka kwenye ngozi ambako hakuwezi kutibika

wanatembea

kuzunguka karibu bila kusudi

Jeremiah 14:19

kukataa

Ili "kukataa" mtu au kitu kinamaanisha kukataa kukubali mtu huyo au kitu. Neno "kukataa" linaweza pia kumaanisha "kukataa kuamini" kitu. Kumkataa Mungu pia inamaanisha kukataa kumtii

Sayuni....Mlima Sayuni

Mwanzo, neno "Sayuni" au "Mlima Sayuni" limeelezea ngome au ngome ambayo Mfalme Daudi alitekwa kutoka kwa Wayebusi. Maneno haya yote yalikuwa njia nyingine za kutaja Yerusalemu.

Mateso

Mateso ni kitendo cha kumsababishia mtu mateso. Mateso ni ugonjwa, huzuni ya kihisia au majanga mengine yatokanayo na mateso. - Mungu aliwapa mateso watu wake kupitia magonjwa na tabu zingine ili kuwasababisha watubu dhambi zao na wamrudie yeye. - Mungu alisababisha mateso au mapigo kwa wana wa Israeli kwa sababu mfalme wao alikataa kumtii Mungu.

kuponya,tiba

Neno "kuponya" na "tiba" zote inamaanisha kumfanya mtu mgonjwa, kujeruhiwa, au ulemavu awe na afya tena.

amani

Neno "amani" linamaanisha hali ya kuwa au hisia ya kuwa hakuna mgogoro, wasiwasi, au hofu. Mtu ambaye ni 'amani' anahisi utulivu na uhakika wa kuwa salama.

hofu

Neno "hofu" linamaanisha hisia ya hofu kali. Ili 'kutisha' mtu ina maana kumfanya mtu huyo awe na hofu sana "Hofu" (au "hofu") ni kitu au mtu anachochea hofu kubwa au hofu. Mfano wa hofu inaweza kuwa jeshi la adui la kushambulia au pigo au magonjwa ambayo yameenea, na kuua watu wengi.

uovu

Neno "uovu" ni neno ambalo ni sawa na maana ya neno "dhambi," lakini inaweza zaidi kutaja matendo ya uovu au uovu mkubwa. Neno "uovu" literally lina maana ya kupotosha au kupotosha (ya sheria). Inahusu uovu mkubwa.

dhambi

Neno "dhambi" linamaanisha vitendo, mawazo, na maneno yanayopinga mapenzi ya Mungu na sheria. Dhambi inaweza pia kutaja kutofanya kitu ambacho Mungu anataka tufanye. Dhambi inajumuisha chochote tunachofanya ambacho hakiitii au kumpendeza Mungu, hata mambo ambayo watu wengine hawajui. Mawazo na vitendo ambavyo haviii mapenzi ya Mungu huitwa "dhambi."

Jeremiah 14:21

Ttaarifa za jumla

Yeremia anaendeleza maombi yake kwa Bwana.

Jeremiah 15

Jeremiah 15:1

Taarifa za jumla

Yeremia amekuwa akimwomba Bwana.

Watoe mbele yangu, ili waweze kuondoka

"watoe mbali nami! Waache wapate! Anarudia wazo hili kwa msisitizo.

Wale wanaotakiwa kufa

"Watu ambao Mungu alisema lazima wafe" au "wale wanaokufa"

Jeremiah 15:3

Taarifa za jumla

Bwana amewaambia kuwa atawatuma baadhi yao kufa, wengine kufa kwa upanga, wengine kufa kwa njaa, na wengine kuwa mateka.

tamko la Bwana

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 1 7.

Nitawafanyia jambo lenye kutisha kwa falme zote za dunia, kwa sababu Manase mwana wa Hezekia, mfalme wa Yuda, alifanya huko Yerusalemu.

Nami nitawafanya kuwa ufalme wa nchi zote kwa sababu ya Manase, mwana wa Hezekia mfalme wa Yuda, huko Yerusalemu.

nitawaweka katika makundi manne

"Nitawaweka makundi manne juu yao"

Jeremiah 15:5

Taarifa ya jumla

Bwana amewaambia kuwa atawapa makundi manne kuwaua-upanga, mbwa, ndege, na wanyama.

Kwa maana ni nani atakayewahurumia, Yerusalemu? Ni nani atakayeomboleza kwa ajili yako? Nani atakayegeuka kuuliza kuhusu ustawi wako?

"Hakuna mtu atakayewahurumia ninyi, watu wanaoishi Yerusalemu. Hakuna mtu anayeweza kuomboleza kwa uharibifu wako. Hakuna mtu anayepaswa kuuliza kwa nini umekuwa watu wenye kusikitisha. "

Umeniacha ... umepata kutoka kwangu

Maneno haya mawili yanamaanisha jambo sawa na kusisitiza kuwa watu wamemwacha Bwana.

kipepeo

chombo cha shamba na kushughulikia kwa muda mrefu na vijiko vya chuma vya mkali, vilivyotumiwa hasa kwa kuinua nafaka kwenye hewa kwa ajili ya kupata.

Nitawafukuza

"Nitawafanya watoto wao afe" au "Nitawaacha maadui wao kuua watoto wao"

Jeremiah 15:8

Taarifa za jumla

Bwana amewaambia kamwe hakuna mtu atakayejali juu yao na kwamba atawaangamiza watu wake kwa sababu hawatageuka njia zao mbaya.

wajane

wanawake ambao waume zao wamekufa

zaidi ya mchanga wa bahari

zaidi ya unavyoweza kuhesabu

kuanguka juu yao

yaliyo wapata

Yeye atakuwa na aibu na kufedheheka

Maneno "aibu" na "kufedheheka" inamaanisha kimsingi kitu kimoja na kusisitiza ukubwa wa aibu. AT "Atakuwa na aibu kabisa."

Jeremiah 15:10

Taarifa za jumla

Katika aya hii, Yeremia anaongea na Bwana juu ya mateso yake, na Bwana anamjibu

Ole wangu, mama yangu

Yeremia anajifanya kuwaambia mama yake kama njia ya kusisitiza jinsi yeye alivyo na huzuni.

mtu wa kushindana na hoja

Maneno '"kushindana" na "hoja" husema kimsingi kitu kimoja. Pamoja wanasisitiza jinsi Yeremia anavyopinga. AT "mtu ambaye kila mtu anasema wakati wote."

kulipa

kutoa mkopo kwa mtu

Je sitakuokoa kwa manufaa?

Jibu thabiti kwa swali hili ni "ndiyo". AT "Nitakuokoa kwa uzuri!"

maadui zako

Wale ni maadui wa Yeremia ambao hawakukubaliana na unabii wake

wakati wa msiba na dhiki

Hapa maneno "msiba" na "dhiki" inamaanisha kimsingi kitu kimoja. Wanasisitiza kiasi au ukubwa wa msiba. AT "wakati wa msiba mkubwa."

Je, mtu anaweza kusaga chuma?

Jibu linalojulikana ni "hapana". Pia, chuma kinawakilisha uamuzi wa hukumu ya Mungu. AT "Hukumu yangu haiwezi kuvunjika, kama vile chuma haiwezi kupasuka"

Hasa chuma kutoka kaskazini iliyochanganywa na shaba?

Swali hili la pili hufanya kwanza kuwa na nguvu zaidi, na hutumia chuma cha nguvu zaidi katika mfano. AT "Zaidi zaidi, hukumu yangu ni kama chuma chenye kigumu"

Jeremiah 15:13

Taarifa za jumla

Katika aya hii, Bwana anasema na taifa la Israeli kama ni mtu mmoja.

utajiri na hazina

Maneno "utajiri" na "hazina" yanamaanisha kitu kimoja na kutaja kitu chochote ambacho watu wanadhani wana thamani.

nyara

vitu ambavyo huiba kutoka mji baada ya kushinda

nchi ambayo huijui

kwa nchi ambayo ni ya ajabu kwako

maana moto utawaka, ukawaka katika ghadhabu yangu juu yako.

Hasira ya Mungu inazungumzwa kama kama ilikuwa moto unaoharibu. AT "Nitawaangamiza kwa sababu nimekasirika sana na wewe"

Jeremiah 15:15

Taarifa za jumla

Yelemia anaongea na Bwana.

Unikumbuke

"Kumbuka mimi" au "Fikiria mimi na hali yangu"

wafuasi wangu

"wale wanaonitafuta kunidhuru"

Katika uvumilivu wako usiniondoe.

"Tafadhali usiendelee kuwavumilia na usiruhusu nife sasa."

Maneno yako yamepatikana

Nimesikia ujumbe wako.

Niliwaangamiza

Nilielewa ujumbe wako

jina lako limetangazwa juu yangu

watu walinitambua kuwa ni mmoja wenu

Jeremiah 15:17

Sikuketi katika mkutano wa

"Sikuwa na muda na"

Kwa nini maumivu yangu yanaendelea na jeraha langu halitibiki, linakataa kuponywa?

"Maumivu yangu yanaendelea na jeraha langu haliwezekani. Siwezi kuponywa."

Je, utakuwa kama maji ya udanganyifu kwangu, maji yanayokauka?

"Ahadi zako kwangu ni kama mkondo ninakwenda kwa ajili ya kunywa tu ili upate kukauka?"

Jeremiah 15:19

utakuwa kama kinywa changu

Yeremia anafananishwa na kinywa cha Bwana kwa sababu atatumiwa kuzungumza ujumbe wa Yahweh. AT "utasema kwa ajili yangu"

wewe mwenyewe

Kitaja, "mwenyewe", kinatumiwa hapa ili kusisitiza amri ilikuwa hasa kwa Yeremia.

kama ukuta wa shaba usiowezekana kwa watu hawa

Bwana anafananisha Yeremia na ukuta kwa sababu watu hawawezi kumshinda.

watapigana vita dhidi yako. Lakini hawatakushinda

"Watapigana nawe, lakini hawatakushinda."

kuokoa......kuwaokoa

Maneno "kuokoa" na "kuwaokoa" yanamaanisha kitu kimoja na kusisitiza usalama ambao Mungu anaahidi.

hili ndilo tamko la Bwana

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 1 7.

kukuokoa kutoka ... na kukukomboa kutoka

Maneno haya yana maana sawa na hutumiwa pamoja ili kusisitiza usalama ambao Mungu hutoa.

mshindani

mtawala ambaye anadai utii kamili na si wa kirafiki kwa watu chini ya utawala wake

Jeremiah 16

Jeremiah 16:1

neno la Bwana lilifika kwa

Tazama jinsi ulivyotafasiri hii katika 1 1.

Watakuwa kama samadi juu ya nchi

Wanaume na binti waliozaliwa katika nchi hulinganishwa na ndovu kwa sababu hawatazikwa baada ya kufa.

Kwa maana wataangamizwa

Hii ni njia nyepesi ya kusema kwamba watakufa.

kwa upanga

Neno "upanga" linamaanisha jeshi la adui.

Jeremiah 16:5

Nimekusanya amani yangu, uaminifu wa agano, na matendo ya huruma huruma

Bwana hukusanya njia tofauti ambazo amewabariki watu wa Israeli kumaanisha kwamba hawatabariki tena watu wa Israeli.

Tamko la Bwana

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 1:7.

wakuu na wadogo

Hii inahusu kila aina ya watu na hutumia ukubwa ili kutaja umuhimu wao. Ama umuhimu mkubwa au umuhimu mdogo.

wala mtu yeyote atawaomboleza. Hakuna mtu atakayejikata au kunyoa vichwa vyao kwa ajili yao

Maneno haya mawili yana maana sawa. Jambo la pili linaimarisha mawazo ya kwanza. AT "Hakuna mtu atakayewaomboleza kwa njia yoyote."

atakayejikata-kata au kunyoa vichwa vyao kwa ajili yao.

Hizi ni desturi ambazo watu walitumia kuonyesha kuwa walikuwa na huzuni sana.

Jeremiah 16:7

Hakuna mtu anayepaswa kugawa chakula chochote wakati wa kuomboleza ili kuwafariji kwa sababu ya vifo, na hawatawapa kikombe cha faraja kwa baba yake au mama yake

Sentensi hizi mbili zina maana sawa. Ilikuwa ni desturi ya kuchukua chakula au divai kwa watu ambao jamaa yao imekufa. Bwana ameondoa faraja yote kutoka kwa watu kwa sababu ya dhambi zao. AT "Usifariji watu wakati wa jamaa wao akifa"

Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 7:3.

Tazama

"Sikiliza" au "Jihadharini na kile nitakachokuambia"

mbele ya macho yako

Hapa neno "yako" ni wingi na linamaanisha watu wa Israeli. AT "mbele yako" au "wapi unaweza kuona"

katika siku zako

""wakati wa maisha yako

sauti ya bwana na bibi

Hii inahusu watu kuadhimisha ndoa.

Jeremiah 16:10

hili ni tamko la bwana

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 1:7.

Maneno "akainama chini" yanamaanisha kimsingi kitu kimoja kama "kuabudu" na inaelezea mkao ambao watu walitumia katika ibada.

Maneno "akainama chini" yanamaanisha kimsingi kitu kimoja kama "kuabudu" na inaelezea mkao ambao watu walitumia katika ibada.

Jeremiah 16:12

Tazama

Neno "tazama" hapa linaongeza mkazo kwa kifuatacho. AT "Kweli"

ukaidi wa moyo wake mbaya

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 11 6.

ambaye anisikiliza

"ambaye anafanya kile ninachomwambia kufanya"

nitawafukuza kutoka nchi hii

"kukufanya uondoke nchi hii"

mchana na usiku

"wakati wote "au" daima "

Jeremiah 16:14

Tazama

Neno "kuona" hapa linaongeza mkazo kwa kifuatacho. AT "kweli"

hili ni tamko la Bwana

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 1:7.

ambapo hawatasema tena

"wakati watu hawatasema tena"

Kama Bwana aishivyo

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 12:16.

Jeremiah 16:16

hili ni tamko la Bwana

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 1:7.

wavuvi wengi.....wawindaji wengi

Bwana anawafananisha watu ambao watawachukua Waisraeli kuwa mateka kwa watu wenye ujuzi wa kunyang'anya mawindo yao.

macho yangu yapo juu ya njia zao zote

"Ninaangalia kila kitu wanachofanya"

hawawezi kujificha mbele yangu

Hapa neno "wao" linaweza kutaja kwa watu au kwa matendo yao. AT "hawawezi kujificha njia zao kutoka kwangu" au "naona yote wanayofanya"

Uovu wao hauwezi kufichika mbele ya macho yangu

"Naona dhambi zao zote"

kujaza urithi wangu na sanamu zao za machukizo

Kifungu hiki kinaelezea "uovu na dhambi" ule ambao watu walifanya.

urithi wangu

Hii inahusu nchi ya Israeli.

Jeremiah 16:19

Bwana, wewe ndiwe ngome yangu

Hapa Yeremia anaanza kuzungumza na Bwana.

ngome yangu, na kimbilio langu, na mahali pa usalama

Yeremia anazungumza juu ya Bwana kama mahali ambako adui hawezi kumshambulia. Anarudia wazo sawa mara tatu.

mwisho wa Dunia

"kila mahali duniani"

baba zetu walirithi udanganyifu

Hapa neno "udanganyifu" linamaanisha miungu ya uongo.

Ubatili mtupu; hakuna faida ndani yao

Hapa maneno "Wao" na "wao" yanataja miungu ya uongo ambayo mababu waliwafundisha kuamini. Maneno mawili yanamaanisha kuwa ni sawa, na pili kuelezea jinsi 'ni tupu.'

Watu hufanya miungu kwa ajili yao wenyewe?

Yeremia anauliza swali hili kusisitiza kwamba watu hawawezi kufanya miungu kwa ajili yao wenyewe. AT "Watu hawawezi kufanya miungu kwa ajili yao wenyewe."

Kwa hiyo tazama!

Hapa Bwana huanza kusema. Neno "tazama" linaongeza mkazo kwa ifuatavyo. AT "Kwa hiyo, kwa kweli,"

Nitawafanya wajue

Hapa neno "wao" linamaanisha watu kutoka mataifa. Bwana anarudia maneno haya kwa msisitizo.

mkono wangu na nguvu zangu

Hapa neno "mkono" linamaanisha nguvu na mamlaka. Maneno mawili yanamaanisha jambo sawa na kusisitiza nguvu kubwa za Bwana. AT "nguvu yangu kubwa."

watajua kwamba Yahweh ni jina langu

Hapa neno "jina" linahusu mtu mzima wa Yahweh. AT "watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wa kweli"

Jeremiah 17

Jeremiah 17:1

Taarifa za jumla

Tazama

Dhambi ya Yuda imeandikwa.....kwenye pembe za madhabahu zako

Ukweli kwamba watu hawaachi kamwe kutenda dhambi hizo hufanya hivyo inaonekana kama rekodi ya dhambi hizo imefunikwa kwenye mioyo yao na madhabahu zao za sanamu.

Dhambi ya Yuda imeandikwa

Hii inaweza kuonyeshwa kwa fomu ya kazi. AT "Watu wa Yuda wameandika dhambi zao"

Imechongwa

Hii inaweza kuonyeshwa kwa fomu ya kazi. AT "Wameiga picha hiyo"

mechongwa kwenye kibao cha mioyo yao

Tabia za dhambi zilizoingizwa za watu zinasemekana kama dhambi zao zimeandikwa kwenye mioyo na akili zao wenyewe. Neno "mioyo" linamaanisha mtu mzima, mawazo yao, hisia, na vitendo. AT "kuchonga katika viumbe vyao"

kwenye pembe za madhabahu zako

Neno "pembe" linamaanisha makadirio kwenye pembe za madhabahu.

kwenye milima ya juu

Baadhi ya matoleo ya kisasa huongeza maneno ya kwanza ya aya ifuatayo kwa maneno haya, kutafsiri "kwenye milima ya juu na milima katika nchi ya wazi."

Jeremiah 17:3

mali yako yote pamoja na hazina zako zote

Maneno "mali" na "hazina" yanamaanisha kitu kimoja na kutaja kitu chochote ambacho wanaona kuwa cha thamani.

nyara

Hii inahusu mambo ambayo watu huiba au kuchukua kwa nguvu.

dhambi iliyo katika maeneo yako yote

"umetenda kila mahali"

urithi

Hii inahusu nchi ya Israeli.

umewasha moto katika ghadhabu yangu, ambao utakawaka milele

Bwana anafananisha hukumu yake na moto unaoharibu. AT "kwa kunifanya niwe mwenye hasira, ni kama umeanza moto ambao utakuunguza"

Jeremiah 17:5

Mtu anayemtegemea mwanadamu amelaaniwa

Mimi nitamlaani mtu yeyote anayeamini kwa wanadamu

amfanyaye mwanadamu kuwa nguvu

Hapa neno "mwili" linamaanisha watu. AT "anamtegemea wanadamu tu kwa nguvu"

kugeuza moyo wake mbali na Bwana

Hapa neno "moyo" linamaanisha mawazo na hisia. AT "anageuza kujitoa kwake mbali na Bwana"

kama kichaka kidogo

Mtu anayemtegemea mwanadamu badala ya Bwana atakuwa kama mmea unaojitahidi kuishi katika ardhi isiyo na rutuba.

nchi isiyozaa

atakuwa bure kama msitu jangwani

Jeremiah 17:7

atakuwa kama mmea karibu na maji

Mtu anayemtegemea Bwana atafanikiwa, kama vile mti unavyofanya wakati unapandwa na mto. Haiathiri wakati hakuna mvua.

Hatawezi kuona joto hilo linalokuja

"Yeye hatasumbuliwa na hali ya hewa ya joto inayokuja"

hawezi kuwa na wasiwasi

hatakuwa na wasiwasi

Jeremiah 17:9

Moyo ni mdanganyifu

Hapa neno "moyo" linamaanisha akili na mawazo ya watu. AT "akili ya binadamu ni udanganyifu zaidi"

ni nani anayeweza kuelewa?

Spika hutumia swali hili kusisitiza kwamba hakuna mtu anayeweza kuelewa moyo wa mwanadamu. AT "hakuna mtu anayeweza kuielewa."

ambaye anajaribu figo

Hisia zinasemwa kama zimezingatia kwenye figo. AT "ambaye hujaribu tamaa za watu"

njia zake

Hapa tabia ya mtu inazungumziwa kama ilivyokuwa njia ambazo anazifuata.

matunda ya matendo yake

Hapa matokeo ya vitendo vya mtu yanazungumzwa kama kwamba yalikuwa matunda ya mti. AT "kile alichofanya"

kama Kware akusanyaye mayai........kuwa tajiri kwa udhalimu

Mfano huu wa ndege unaokwisha mayai ya ndege mwingine una maana ya kuonyesha mtu tajiri ambaye hufanya fedha zake kwa kuiba wengine.

wakati nusu ya siku zake ukipita

Hapa "siku" zinasimama kwa maisha yote ya mtu. AT "wakati aliishi nusu tu ya maisha yake"

utajiri huo utamuacha

Utajiri huzungumzwa kama watumishi ambao wangemuacha mmiliki wao. AT "atafungua utajiri wake"

mwishowe

"mwisho wa maisha yake"

atakuwa mpumbavu

"ataonyeshwa kuwa mpumbavu"

Jeremiah 17:12

Mahali pa hekalu letu ni kiti cha enzi

Yeremia anafananisha hekalu na "kiti cha enzi cha utukufu" kwa sababu kuna pale ambapo Bwana anakaa na kutawala.

Mahali pa hekalu letu

Hii inamaanisha Sayuni huko Yerusalemu.

Wote ambao wanakuacha

Hapa neno "wewe" linamaanisha Bwana.

Wale walio katika nchi ambao wanageuka kutoka kwakowatauliwa

"Wewe utawaangamiza wale walio katika nchi ambao hugeuka kutoka kwako"

chemchemi ya maji yaliyo hai

Yeremia anafananisha Bwana na chemchemi ya maji safi. AT "chemchemi ya maji safi, ya maji" au "chanzo cha maisha yote"

Nitaponywa ... Nitaokolewa

"hakika utaniponya ... utakuwa umenipenda"

wimbo wangu wa sifa

"ambaye nitamsifu"

Jeremiah 17:15

tazama

"Angalia" au "Sikiliza" au "Jihadharini na kile ninachokuambia"

wao wananiambia

Hapa neno "mimi" linamaanisha Yeremia na neno 'wao' kwa adui zake.

Neno la Bwana liko wapi?

Watu wanatumia swali hili kumtukana Yeremia kwa sababu mambo ambayo alisema hakujawahi kutokea. AT "Ambapo ni vitu gani ambavyo Bwana alikuambia utatokea?" au "Mambo ambayo Bwana alikuambia utatokea hayakufanyika."

Hebu lije

"Waache wapate"

mchungaji akufuatae

Bwana alimuita Yeremia kuwaongoza watu, kama mchungaji anavyoongoza kondoo wake.

Sikuitamani

Sikuhitaji

matangazo yaliyotoka midomoni mwangu

"maagizo niliyosema" au "mambo niliyotangaza"

Yalifanyika

"Nimewafanya"

Jeremiah 17:17

siku ya msiba

"Siku" inawakilisha muda wa hukumu ya Mungu kufanyika. AT "wakati wa msiba"

Waaibike watu wanaoniudhi, lakini nisiaibike mimi

"Kuniitia aibu juu ya wafuasi wangu, lakini usinitie aibu"

Watafadhaika, lakini usiache nifadhaike

Kifungu hiki kimamaanisha kimsingi kitu kimoja na kilichopita na kinatumika kwa msisitizo. AT "Kuwafanya wawe na hofu sana, lakini usinifanye kuwa hofu"

kuwaangamiza maradufu

"kuwaangamiza kwa uharibifu kamili" au "kuwaangamiza mara mbili zaidi"

Jeremiah 17:19

Bwana

Neno "Bwana" ni jina la Mungu ambalo lilifunua wakati alipoongea na Musa kwenye kichaka kilichowaka. Jina "Bwana" linatokana na neno linamaanisha, "kuwa" au "kuwepo." Maana iwezekanavyo ya "Bwana" ni pamoja na, "yeye ni" au "Mimi" au "yule anayefanya kuwa."

Lango, Bango la lango

"Lango" ni kizuizi kinachotiwa nguzo kwenye eneo la kufikia kwenye uzio au ukuta unaozunguka nyumba au jiji. "Bango la lango" linamaanisha mbao ya mbao au ya chuma ambayo inaweza kuhamishwa mahali pa kufunga lango. Lango la jiji linaweza kufunguliwa ili kuruhusu watu, wanyama, na mizigo kusafiri na nje ya mji.

mfalme

Neno "mfalme" linamaanisha mtu ambaye ndiye mtawala mkuu wa mji, serikali, au nchi. Mfalme huchaguliwa kutawala kwa sababu ya uhusiano wa familia na wafalme wa zamani. Wakati mfalme akifa, huwa ni mwanawe mkubwa ambaye huwa mfalme wa pili.

Yuda, Ufalme wa Yuda

Kabila la Yuda ilikuwa kubwa zaidi katika kabila kumi na mbili za Israeli. Ufalme wa Yuda ulijengwa na kabila za Yuda na Benyamini. Mji mkuu wa ufalme wa Yuda ulikuwa Yerusalemu. Wafalme nane wa Yuda walimtii Bwana na kuwaongoza watu kumwabudu. Wafalme wengine wa Yuda walikuwa wabaya na wakawaongoza watu kuabudu sanamu

Yerusalemu

Yerusalemu ilikuwa ni mji wa kale wa Wakanaani ambao baadaye ulikuwa mji la muhimu sana katika Israeli. Iko karibu kilomita 34 magharibi ya Bahari ya Chumvi na kaskazini mwa Bethlehemu. Bado ni mji mkuu wa Israeli wa sasa. Jina, "Yerusalemu" linalotajwa kwanza katika kitabu cha Yoshua. Majina mengine ya Agano la Kale kwa mji huu ni pamoja na 'Salem', "jiji la Jebus," na "Sayuni." "Yerusalemu" na "Salem" wote wana maana ya "amani." Yerusalemu ilikuwa awali ngome ya Yebusi inayoitwa "Sayuni" ambayo Mfalme Daudi alitekwa na kuiweka katika jiji lake kuu.

neno la Mungu, neno la Bwana, neno la Bwana, maandiko

Katika Biblia, neno "neno la Mungu" linamaanisha chochote ambacho Mungu amewaelezea watu. Hii ni pamoja na ujumbe uliozungumzwa na ulioandikwa. Yesu pia huitwa "Neno la Mungu." Neno "maandiko" linamaanisha "maandiko." Inatumika tu katika Agano Jipya na inahusu maandiko ya Kiebrania au "Agano la Kale." Maandishi haya yalikuwa ujumbe wa Mungu kwamba alikuwa amewaambia watu kuandika ili miaka mingi katika siku zijazo watu waweze kuisoma. Maneno yanayohusiana ya "Yahweh" na "neno la Bwana" mara nyingi hutaja ujumbe maalum kutoka kwa Mungu ambao ulitolewa kwa nabii au mtu mwingine katika Biblia.

Jeremiah 17:21

kwa ajili ya maisha yenu

"kulinda maisha yako" au "ikiwa unathamini maisha yako"

Hawakusikiliza wala kutaega masikio yao

Maneno haya mawili yanamaanisha jambo sawa na kusisitiza kuwa watu walikataa kusikiliza. AT "Walikataa kusikiliza" au "Walikataa kutii."

Jeremiah 17:24

Hili ni tamko la Bwana

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 1:7.

ambae amekaa kiti cha Daudi

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 13:12.

mji huu utakaa milele

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "watu watakaa jiji hili milele"

Jeremiah 17:26

nitawasha moto katika malango yake

"Nitaanza moto katika milango ya Yerusalemu"

ambayo hayawezi kuzima

kwamba watu hawawezi kuzima

Jeremiah 18

Jeremiah 18:1

Hii ndio neno la Bwana ambalo lilikuja

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 1:1.

nyumba ya mfinyanzi

Mfinyanzi ni mtu ambaye hufanya sufuria na vitu vingine muhimu, vidogo kutoka kwenye udongo. AT "semina ya mfinyanzi"

tazama

Neno "tazama" linatujulisha mtu mpya katika hadithi. Lugha yako inaweza kuwa na njia ya kufanya hivyo.

gurudumu la mfinyanzi

Gurudumu la mfinyanzi ni meza ndogo ambayo inazunguka, mtungi hutumia kutengeneza sufuria. AT "kwenye meza yake" au "kutengeneza sufuria"

kutengeneza

"kutengeneza" au "kuunda"

iliharibika mkononi mwake

"akaanguka mkononi mwake"

kwa hiyo alibadili mawazo yake

hivyo alifanya uchaguzi tofauti

nzuri machoni pake

Macho husimama kwa mfinyanzi mwenyewe. AT "mzuri kwake"

Jeremiah 18:5

neno la Bwana lilikuja

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 1:1.

Je, siwezi kuwa kama huyu mfinyanzi kwenu, nyumba ya Israeli?

Kwa swali hili, Bwana anasisitiza mamlaka yake ya kufanya kama yeye apendezwavyo na Israeli. AT "Naruhusiwa kutenda kwako, nyumba ya Israeli, kama mfinyanzi anafanyavyo juu ya udongo"

hili ni tamko la Bwana

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 1:1.

Angalia

Neno "kuona" hapa linaongeza mkazo kwa ifuatavyo. AT "Hakika!"

Kama udongo katika mkono wa mfinyanzi-ndivyo ulivyo mkononi mwangu

Kifungu hiki kinarudia kile kilichoingizwa katika maneno ya awali kwa namna ya mfano.

ninaweza kutangaza jambo

"labda mimi kutangaza kitu" au "kwa mfano, mimi kutangaza kitu"

kuuvunja, au kuuharibu

Maneno haya mawili yanamaanisha kitu kimoja na kusisitiza jinsi hukumu ya Mungu itaharibika.

nitaondoka

"kuzuia" "kuacha"

Jeremiah 18:9

nitaujenga au kuupanda

Hizi vitenzi viwili kimsingi inamaanisha kitu kimoja na kusisitiza baraka za Mungu.

kuupanda

Kifungu hiki kinalinganisha baraka za Mungu kwa kuuweka kwa makini mmea katika bustani

mabaya machoni pangu

Macho ya Bwana hutaja kwa Yahweh mwenyewe. AT "mambo ambayo nadhani ni mabaya" au "mabaya kulingana na mimi"

kutosikiliza sauti yangu

"wasioti amri zangu" au "wasiozingatia kile nilichosema"

Jeremiah 18:11

Angalia

"Angalia" au "Sikiliza" au "Jihadharini na kile ninachokuambia"

Mimi ni karibu kuunda maafa dhidi yako. Mimi ni karibu kupanga mpango dhidi yenu

Maneno haya yote yanaelezea kitu kimoja ili kusisitiza ni hatari gani ya onyo hili.

fanya maafa

Bwana anaelezea maafa kama kitu ambacho anapanga kama mtu atakavyofanya udongo. AT "sura" au "kuunda"

kupanga

"fikiria" au "mpango" au "kuunda"

njia zake mbaya

"njia yake mbaya ya kuishi"

jia zako na matendo yako

Maneno "njia" na "matendo" kimsingi yanamaanisha kitu kimoja na kusisitiza kwamba njia yao yote ya maisha inabadilika.

Lakini watasema

Neno "wao" linamaanisha wenyeji wa Yuda na Yerusalemu.

Hili halina maana

Hatuna matumaini

uovu wake, matamanio ya moyo

Mtu huyu anatambulika na sehemu ya mwili wake unaohusishwa na hisia. AT "kwa tamaa zake mbaya"

Jeremiah 18:13

Uliza watu wa mataifa, ambao wamewahi kusikia habari kama hii?

Swali hili linamaanisha taarifa. AT "Hakuna mahali popote duniani ambaye mtu yeyote amewahi kusikia jambo kama hili."

Bikira wa Israeli

Ilikuwa ya kawaida kutaja mataifa kama kama walikuwa wanawake. Hata hivyo, "bikira" hufanya mtu kufikiri juu ya mwanamke mdogo ambaye hajawahi kuolewa na hivyo hakuwahi kuwa na nafasi ya kuwa na imani kwa mumewe. Kwa hiyo, kumwita Israeli bikira ni matumizi ya ajabu ya lugha. AT "Israeli, ambaye hujifanya uongo kuwa kikamilifu kujitoa kwa Mungu"

Je, theluji ya Lebanoni imetoka milima yenye miamba juu ya pande zake?

Swali hili linamaanisha taarifa. AT "theluji ya Lebanoni hakika kamwe huacha milima yenye miamba juu ya pande zake"

Je, mito ya mlima inayotoka mbali iliharibiwa

Swali hili linamaanisha taarifa. AT "Hakuna chochote kinachoweza kuharibu mito hiyo ya mlima inayotoka mbali."

Jeremiah 18:15

mashaka katika njia zao

Hapa neno "yao" linamaanisha "watu wangu."

itakuwa ya hofu

"itakuwa kitu ambacho kinatisha watu"

kupiga kelele

Hii ni sauti inayoonyesha kukataa kwa nguvu.

atakayepita karibu naye

Hapa neno "yake" linamaanisha "Nchi yao."

Nitawaangamiza mbele ya adui zao kama upepo wa mashariki.

Bwana anajilinganisha na upepo kutoka mashariki ambayo hugawa majivu na uchafu.

Nitawaangamiza

Hapa neno "yao" linamaanisha "watu wangu."

Nitawageuzia kisogo, wala sio uso wangu

Hatua hii inaashiria kwamba Mungu atakataa kuwasaidia watu wake.

Jeremiah 18:18

tufanye njama dhidi ya Yeremia

"hebu tufanye mipango ya kumdhuru Yeremia"

maana sheria haitapotea kabisa kwa makuhani, wala ushauri kutoka kwa wenye hekima, au maneno ya manabii

"makuhani watawa na sheria daima, watu wenye busara watawapa ushauri daima, na manabii daima watazungumza"

shambulie kwa maneno yetu

"sema mambo ambayo yatamdhuru"

Nisikilizeni

Hapa Yeremia anaanza kuzungumza na Bwana.

Je, maafa kutoka kwao itakuwa malipo yangu kwa kuwa mema kwao?

Yeremia anauliza swali hili kusisitiza kwamba vitendo vyema havipaswi kulipwa kwa mambo mabaya. AT "Maafa kutoka kwao hawapaswi kuwa tuzo yangu kwa kuwa mazuri kwao."

wamenichimbia shimo

"chimba shimo kunipiga na kuniua"

ili kusababisha hasira yako kugeuka mbali nao

"ili usiwaadhibu kwa hasira yako"

Jeremiah 18:21

uwatie mikononi mwa wale wanaotumia upanga

"Upanga" unawakilisha vita. "Kwa sababu ya kufa katika vita"

waache wanawake wao wafiwe na kuwa wajane

"waache watoto na waume wa wake zao wafe"

watu wao watauawa, na vijana wao wauawe kwa upanga

"watu huua watu wao, na kuwaua vijana wao kwa upanga"

Kelele ya kusikitisha isikiwe

"watu husikia sauti ya shida"

Kwa kuwa wamechimba shimo kunikamata na wameficha mitego katika miguu yangu

Adui wa Yeremia wanajaribu kumkamata kama mtu angeweza kukamata wanyama wa mwitu. Yeremia anarudia wazo sawa mara mbili kwa msisitizo.

wamechimba shimo

Angali jinsi ulivyotafasiri hii katika 18:18.

Usiondoe dhambi zao mbali nawe

Maneno haya inamaanisha kitu kimoja kama maneno ya awali.

waache waangamizwe mbele yako

"watu wawaangamizwe mbele yako"

Jeremiah 19

Jeremiah 19:1

Bonde la Ben Hinomu

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 7:31.

Angalia

"Sikiliza" au "Jihadharini na kile nitakachokuambia"

masikio ya kila mtu anayesikia yatawaka

"itamshangaza kila mtu anayeisikia"

Jeremiah 19:4

wameniacha

Hapa neno "wao" linamaanisha watu wa Yuda.

wamejaza mahali damu isiyo na hatia

""aliuawa watu wengi wasio na hatia mahali hapa"

kitu ambacho sijawaamuru

"kitu ambacho ninawazuia kufanya"

wala hakuingia ndani ya akili yangu

Hapa neno "akili" linamaanisha mawazo ya Bwana. AT "wala sijawahi kufikiri juu yake"

Jeremiah 19:6

Angalia

"kusikiliza" au "kuwa makini na kile ninachokuambia"

hili ni tamko la Bwana

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 1:7.

mahali hapa hapataitwa tena

"watu hawataita tena mahali hapa"

Tofethi....bonde la Ben Hinomu....bonde la machinjo

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 7:31.

Nitawafanya wapate kuuawa kwa upanga mbele ya adui zao

"Nitawafanya maadui wao kuwaua kwa mapanga"

kwa mkono wa wale wanaotafuta maisha yao

Maneno haya yanamaanisha kimsingi kitu kimoja kama maneno ya awali. AT "Nitawawezesha wale ambao wanataka kuwaua kuwaua"

milele

"S" sauti, ambayo inaonyesha kukataa kwa nguvu.

Nitawafanya kula

"Nitawafanya watu wanaokaa Yerusalemu kula"

Jeremiah 19:10

hili ni tamko la Bwana

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 1:7.

isiweze isiweze kutengenezwa tena tena

"hakuna mtu anayeweza isiweze kutengeneza tena"

Jeremiah 19:12

hili ni tamko la Bwana

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 1:7.

wafalme wa Yuda

"na nyumba za wafalme wa Yuda"

Jeremiah 19:14

Angalia

"Sikiliza" au "Jihadharini na kile nitakachokuambia"

walishupaza shingo zao na kukataa kusikiliza

Maneno "kukataa kusikiliza" ina maana kimsingi kitu kama "shingo la shingo" na kuelezea jinsi watu walivyofanya hivyo.

Jeremiah 20

Jeremiah 20:1

Taarifa za jumla

Angalia

alikuwa msimamizi mkuu

Hapa neno "yeye" linamaanisha Pashuri.

Pashuri akampiga Yeremia

Inawezekana maana ni 1) kwamba Pashuri mwenyewe alimpiga Yeremia au 2) Pashuri aliwaamuru watu wengine kumpiga Yeremia.

masanduku

Hifadhi ni sura ya mbao na mashimo ambayo watu hutumia kuifunga mikono, miguu, na kichwa cha mfungwa.

Lango la juu la Benyamini

Lango hili ni tofauti na lango katika ukuta wa jiji ambalo lilikuwa na jina sawa.

Jeremiah 20:3

Ikawa

Kifungu hiki kinatumiwa hapa kuonyeshwa ambapo hatua huanza. Ikiwa lugha yako ina njia ya kufanya hivyo, unaweza kufikiria kuitumia hapa.

wewe ni Magor-Misabibu

Jina hili linamaanisha "hofu kwa kila upande" au "kuzungukwa na hofu."

Tazama

"Jihadharini na kile nitakachokuambia"

wataanguka kwa upanga wa adui zao

"adui zao watawaua kwa mapanga"

macho yako yataona

"utaiona"

Nitawatia Yuda mkononi mwa mfalme wa Babeli

Hapa neno "mkono" linamaanisha nguvu. AT "Nitamuwezesha mfalme wa Babeli kuishinda Yuda wote"

Jeremiah 20:5

Nitampa

Hapa neno "yeye" linamaanisha mfalme wa Babeli.

utajiri wote ... utajiri wake wote, vitu vyote vya thamani na hazina zote

Bwana anarudia wazo moja la msingi mara nne kwa msisitizo. Hiyo ni Babeli itachukua utajiri wote wa Israeli, ikiwa ni pamoja na mali ya Mfalme.

Nitaweka vitu hivi mikononi mwa adui zako

Hapa neno "mkono" linamaanisha kuwa milki. AT "Nitawaacha maadui wako kuchukua milki ya vitu hivi" au "Nitawapa vitu hivi kwa adui zenu"

Wewe na wapendwa wako wote ambao uliwatabiria maneno ya uongo mtazikwa huko

"Huko, watu watakuzika wewe na wapendwa wako wote ambao uliwatabiria mambo ya uongo"

Jeremiah 20:7

Taarifa za jumla

Yeremia anaongea na Bwana

hakika nilikuwa nimedanganywa

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "Wewe hakika umenidanganya" (UDB) au "umenidanganya"

Wewe umenidanganya, Bwana. Kwa hakika nilikuwa nimedanganywa

Baadhi ya matoleo ya kisasa yanatafsiri maneno haya ya Kiebrania kama "Wewe umenishawishi, Bwana. Kwa hakika nilikuwa na ushawishi.

kuchekesha

Huyu ni mtu ambaye wengine wanamcheka na kumchukiza.

Watu wananidharau kila siku, siku zote

Maneno haya yanamaanisha kimsingi kitu kimoja kama maneno ya awali.

nimeita na kutangaza

Maneno haya mawili yanamaanisha jambo sawa na kusisitiza kwamba alitangaza ujumbe wa Bwana kwa ujasiri. AT "alitangazwa kwa wazi" au "alitangaza kwa sauti kubwa"

neno la Bwana limefanywa shutumu na dhihaka kwangu kila siku

Hapa "neno" linamaanisha ujumbe wa Bwana. AT "Watu wana nishutumu na kunidhihaki kila siku kwa sababu mimi hutangaza ujumbe wa Bwana"

shutumu na dhihaka

Maneno "kutukana" na "kunyosha" inamaanisha kuwa sawa na kusisitiza kwamba watu wamemcheka Yeremia kwa kutangaza ujumbe wa Bwana. AT "sababu ya watu kunidharau"

Sitatangaza tena jina lake

Inawezekana maana ni 1) "Sitasema tena juu yake" (UDB) au 2) "Sitasema tena kama mjumbe wake"

Ni kama moto moyoni mwangu, uliofanyika ndani ya mifupa yangu

Yeremia anazungumzia ujumbe wa Bwana kama ni moto usio na udhibiti. AT "neno la Bwana ni kama moto unaowaka ndani yangu"

Jeremiah 20:10

Lazima tumshitaki

Adui wa Yeremia wanasema maneno haya.

Labda anaweza kudanganywa.....kujilipiza kisasi kwake

Adui wa Yeremia wanasema maneno haya.

Labda anaweza kudanganywa

"Pengine tunaweza kumdanganya"

Bwana yu pamoja nami kama mpiganaji mwenye nguvu

Bwana ni kama shujaa mwenye nguvu ambaye humlinda Yeremia na kuwashinda adui zake.

hawawezi kusahau kamwe

"watu hawatasahau kamwe"

Jeremiah 20:12

ambao wanaona akili na moyo

"ni nani ajuaye watu wanadhani na wanataka"

ameokoa maisha ya wale waliokandamizwa

"aliwaokoa watu waliokandamizwa"

kutoka kwenye mikono ya waovu

Hapa neno mkono linamaanisha nguvu. AT "kutoka kwa nguvu ya waovu"

Jeremiah 20:14

Taarifa za jumla

Yeremia anaendelea kuzungumza na Bwana.

Na ilaaniwe siku niliyozaliwa

"Laana siku nilipozaliwa"

Usiruhusu siku ambayo mama yangu alinizaa ibarikiwe

"Usiibariki siku ambayo mama yangu alinizaa."

Na alaaniwe mtu aliyemwambia baba yangu

"Mlaani mtu aliyemwambia baba yangu"

Jeremiah 20:16

mtu yule

Hii inahusu mtu aliyemwambia baba wa Yeremia ya kuzaliwa kwa Yeremia.

miji ambayo Bwana aliiangamiza

Hii inahusu Sodoma na Gomora.

hakuwa na huruma

Hapa neno "yeye" linamaanisha Bwana.

Yeye kusikia sauti ya msaada

apa neno "yeye" linamaanisha "mtu yule"

kumfanya mama yangu kaburi langu

Tumbo la mama yake Yeremia lingekuwa limehifadhi mwili wake mfu kama kaburi linavyoweka mwili wa marehemu.

Kwa nini nilitoka tumboni ili kuona matatizo na uchungu.....aibu?

Yeremia anatumia swali hili kulalamika kwamba hapakuwa na sababu nzuri ya kuzaliwa. AT "Hakukuwa na sababu ya mimi kuzaliwa tu kuona matatizo na uchungu ... aibu."

kuona matatizo na uchungu

Maneno "matatizo" na "uchungu" inamaanisha kuwa ni sawa na kusisitiza kiasi na ukali wa mateso. AT "kupata uzoefu mkubwa wa mateso."

siku zangu zimejaa aibu

"maisha yangu yamejaa aibu"

Jeremiah 21

Jeremiah 21:1

Taarifa za jumla

Angalia

Pashuri

Hii sio Pashuri ambae ameetajwa katika 20:1

Pata ushauri kutoka kwa Bwana kwa ajili yetu

"Tafadhali sema na Bwana kwa ajili yetu. Mwambie kama atatusaidia "

kama zamani

"kama alivyofanya zamani"

kumfanya aondoke kwetu

"atamfanya aende"

Jeremiah 21:3

vyombo vya vita vilivyo mkononi mwenu

"askari unaowaamuru"

kukufunga

"kuja karibu na wewe"

kwa mkono ulioinua na mkono wenye nguvu

Maneno haya yote ni maneno ya kiidioma ambayo yanataja nguvu kubwa. AT "na nguvu kubwa sana."

ukali, ghadhabu, na hasira kubwa

Maneno haya yote yanamaanisha kimsingi kitu kimoja. Pamoja wanasisitiza ukubwa mkubwa wa hasira yake. AT "kwa hasira kubwa sana."

Jeremiah 21:6

Taarifa za jumla

Angalia

wenyeji wa mji huu

"wale wanaoishi Yerusalemu"

Jeremiah 21:8

watu hawa

"watu wa Yerusalemu"

nitaweka mbele yako njia ya uzima na njia ya mauti.

Bwana anawapa watu wa Yerusalemu uchaguzi ambao utaamua kama wanaishi au kufa.

kuanguka kwa magoti mbele

"kujisalimisha kwa "

imefungwa kinyume

"kushambuliwa kutoka pande zote"

Nimeweka uso wangu kinyume

"Nimekataa kupinga" au "nimegeukia"

Yeye ataokoka na maisha yake

Yule anayejisalimisha kwa Wababiloni ataokoka na maisha yake, ingawa atapoteza mali zake zote.

hili ni tamko la Bwana

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 1:7.

Jeremiah 21:11

Kuhusu nyumba ya mfalme wa Yuda, sikiliza neno la Bwana

"Sikiliza yale Bwana asema juu ya mfalme wa Yuda, familia yake, na watumishi wake."

Hukumuni kwa haki asubuhi

"Daima uwatendee watu ambao unatawala juu ya haki"

mkono wa mwenye kuonea

"nguvu ya yule anaonea"

"Nitawaadhibu na kuharibu katika ghadhabu yangu haraka na kabisa"

"Nitawaadhibu na kuharibu katika ghadhabu yangu haraka na kabisa"

Jeremiah 21:13

Mimi ni juu yako, mwamba wa bahari

"Ninakupinga, Yerusalemu" au "Nitawaadhibu, watu wa Yerusalemu"

hili ni tamko la Bwana

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 1:7.

'Ni nani atashuka kutupiga?...Ni nani atakayeingia kwenye nyumba zetu?

"Hakuna yeyote atushambulia na hakuna mtu atakayeingia nyumba zetu"

Nitawaadhibu kutokana na matunda ya matendo yako

"Nitakudhibu kama unavyostahiki kwa sababu ya mambo uliyoyatenda"

matokeo ya matendo yako

"matokeo ya matendo yako"

Jeremiah 22

Jeremiah 22:1

kiti cha Daudi

Hii ina maana ya kuwa na mamlaka ya kifalme, kama vile Daudi alivyokuwa nayo. AT "kutawala kama mfalme, kama Daudi mbele yenu"

kusikiliza neno la Bwana

"kuwa makini kwa neno la Bwana"

wewe na watumishi wako, na watu wako

"wewe na watumishi wako, na watu wako wanaoishi katika nchi yake"

mnaokuja kwa malango haya

Haya ni malango ya jumba la mfalme. AT "ambaye anakuja kumtembelea mfalme"

mkono wa mshindani

Neno "mkono" linamaanisha nguvu au udhibiti wa mtu.

Usimtendee mabaya

Usimtendee mtu vibaya

yatima

mtoto ambaye hana wazazi

Usifanye......kumwaga damu isiyo na hatia

"Usifanye ... kuwaua watu wasio na hatia"

mahali hapa

"mahali hapa" linamaanisha Yerusalemu, au hata nchi nzima ya Yuda. Hii haina maana kuwa ni vizuri kuua watu katika maeneo mengine.

Jeremiah 22:4

wafalme wanaoketi kiti cha Daudi

Hii inahusu wafalme wenye mamlaka kama Daudi. Wafalme, wanatawala kama Daudi mbele yao

wakiendesha gari na farasi

Maneno haya yanaelezea wafalme kama wenye nguvu na matajiri.

yeye, watumishi wake, na watu wake

Sentensi hii inaorodhesha wote ambao watakuwa na nguvu na matajiri. "yeye, watumishi wake, na watu wake watapanda ngome juu ya magari na farasi"

ikiwa husikiliza

"ikiwa husikiliza" (UDB) au "ikiwa hutii"

hili ni tamko la bwana

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 1:7.

Jeremiah 22:6

nyumba ya mfalme wa Yuda

Hii pia inaweza kutafsiriwa kama "nyumba ya mfalme wa Yuda" na inahusu familia na wazao wa Mfalme wa Yuda.

Wewe uko kama Gileadi, au kama kilele cha Lebanoni

Bwana anaelezea hisia zake nzuri kwa familia na wazao wa Mfalme wa Yuda

nitakugeuza kuwa jangwa

"kwa sababu miji yako kuwa tupu au isiyoishi"

Jeremiah 22:8

Kisha mataifa mengi yatapita kwenye mji huu

"Kisha watu wengi kutoka mataifa mbalimbali watapita kwenye mji huu."

wakainama kwa miungu mingine, wakaiabudu

Maneno haya mawili yanamaanisha kitu kimoja. Maneno "akainama chini" yanaelezea mkao ambao watu walitumia katika kuabudu.

Jeremiah 22:10

Taarifa za jumla

Msemaji wa Bwana amebadilishana na kumwambia mfalme wa Yuda na sasa anazungumza na wasikilizaji kwa ujumla.

kuiona nchi aliyozaliwa tena

"angalia nchi ya Israeli tena" au "kuangalia nchi yake tena"

Jeremiah 22:11

Yehoahazi

Jina kwa Kiebrania ni "Shalum," lakini anajulikana zaidi kama Yehoahazi.

Jeremiah 22:13

nyumba

Nyumba inatumika hapa kuelezea Yehoyakimu na familia yake.

Jeremiah 22:15

e, hii ndiyo inakufanya uwe mfalme mzuri, kwamba unataka kuwa na mbao za mwerezi

"Kuwa na nyumba ya mwerezi haifanyi iwe mfalme mzuri"

Je baba yako hakula na kunywa..... haki?

"Mfalme Yosia alifurahia maisha yake ... haki."

Je! Hii sio maana ya kunijua?

"Hii ndiyo maana ya kunijua mimi."

Jeremiah 22:17

hakuna kitu katika mmacho na moyo wako

"hakuna kitu katika mawazo yako na hisia"

faida yako

Hii ni kupata pesa kwa kudanganya au kwa kutumia njia zisizofaa.

kumwaga damu isiyo na hatia

"kuua watu wasio na hatia"

kuwafanyia jeuri wengine

"kufanya vurugu kwa wengine ili kupata fedha"

Ole, ndugu yangu! ...... Ole, dada yangu!.....Ole, bwana!....Ole, utukufu!

Bwana hutumia neno "Ole" mara kadhaa kwa msisitizo. Anawaambia watu mbalimbali ambao kwa kawaida wataonyesha huzuni kubwa wakati mtu anapokufa.

Atazikwa maziko ya punda, ataburuzwa mbali na kutupwa nje

"Watauzika mwili wa marehemu kama ambavyo wanaweza kumzika punda aliyekufa; watauburuza na kuutupa nje"

Jeremiah 22:20

Paza sauti yako

"Piga kelele Bashani"

milima ya Abarimu

Angalia

Nilinena nawe wakati ulioko salama

"Nilinena na wewe unapokuwa ukifanya vizuri"

Hii ilikuwa desturi yako

"Hii ndiyo njia yako ya maisha"

hukusikiliza sauti yangu

"hamkunitii"

Jeremiah 22:22

Upepo utawalisha wachungaji wako wote

"Viongozi wako wataondolewa"

Nyumba ya Msitu wa Lebanoni, wewe ambaye ni kiota kati ya mierezi

"nyumba iliyotengenezwa kutoka kwa mierezi ya Lebanoni"

jinsi utakavyohurumiwa wakati uchungu wa maumivu ya huzuni yanavyokujia kama unatakakuzaa

"utasihi kwa sababu ya maumivu yako"

Jeremiah 22:24

Kama mimi niishivyo

"Hakika"

ata kama wewe, Konia, mwana wa Yehoyakimu....ulikuwa alama ya mkono wangu wa kulia, ningekuangusha

"Ikiwa wewe, Yehoyakini ... ulikuwa alama ya mkono wangu wa kulia, ningekuchota mkono wangu" au "Yehoyakimu ... hata kama wewe ndio mfalme niliyechagua kama uonyesho wa nguvu zangu, mimi ingekuwa bado adhabu yenu"

Nimekutia mikononi mwa wale wanaotafuta maisha yako

"Nimewafanya iwezekanavyo kwa wale wanaotaka maisha yako kukupeleka"

Jeremiah 22:27

nchi hii ambayo watataka kurudi

Inaelezea nchi ya Yuda

Je! Hii ni chombo kilichodharauliwa na kilichopasuka? Je, mtu huyu Yehoyakini ni chombo kisichomfurasha mtu?

"Yehoyakini haufai na hakuna mtu anayefurahi naye."

Kwa nini wamemtupa yeye na wazao wake, kumpeleka katika nchi wasiyoijua?

"Watu wanapaswa kuwaondoa Yehoyakini na familia yake kutoka nchi"

Jeremiah 22:29

Nchi, Nchi, Nchi

Bwana anaongea ujumbe wake kwa watu wote wa nchi kwa kuitaja nchi wanayoishi.

Sikieni neno la Bwana

"tii neno la Bwana"

Jeremiah 23

Jeremiah 23:1

wachungaji ambao huangamiza na kuwatawanya kondoo wa malisho yangu

Bwana anaelezea Israeli kama malisho yake, watu wa Israeli kama kondoo wake na viongozi wao katika Israeli kama wachungaji.

Tamko la Bwana

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 1:7.

mnawatawanya kundi langu na kuwafukuza

Maneno haya mawili yana maana sawa. Jambo la pili linaimarisha mawazo ya kwanza.

kulipa kwa uovu

Bwana inahusu matendo mabaya kama mkopo uliopatiwa na unaweza kulipwa. AT "kulipiza kisasi kwa uovu"

Jeremiah 23:3

Taarifa za jumla

Bwana anaendelea kusema juu ya watu wa Israeli kama kondoo wake na viongozi wa Israeli kama wachungaji

kwenye eneo la malisho

"ambapo mahitaji yao yote yatatolewa"

ambako watazaa na kuongezeka

Neno "ongezeko" linaelezea jinsi watakavyokuwa "wenye kuzaa." AT "wataongezeka kwa idadi kubwa."

hivyo hawataogopa tena au kupotezwa

Maneno "yamevunjwa" inamaanisha kwamba mtu amewafanya waogope na maana yake ni sawa na "hofu." "Hakuna mtu atakayewaogopa tena."

Hakuna hata mmoja

"Hakuna kati ya watu wangu"

Jeremiah 23:5

siku zinakuja

Wakati ujao unasemwa kama ni kitu kinachoja kwa msemaji au wasikilizaji. AT "wakati utafanyika"

Tamko la Bwana

"nini Bwana ametangaza" au "nini Bwana amesema." Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 1:7.

tawi la haki

Mfalme huyu wa baadaye alitoka kwa Daudi anazungumzwa kama kwamba alikuwa tawi iliyopandwa kwenye mti. AT "mwana wa haki"

tawi la haki

Baadhi ya matoleo ya kisasa yanatafsiri "mrithi halali wa kiti cha enzi."

hukumu na haki katika nchi

"hukuimu" na "haki" husimama kwa watu wanaofanya kwa haki na kwa haki. "Kwa sababu watu kutenda kwa haki na kwa haki "

katika nchi

Hapa "nchi" inawakilisha watu wote katika taifa hilo. AT "kwa watu wote katika taifa"

Yuda ataokolewa, na Israeli wataishi kwa usalama

Sentensi hizi mbili zina maana sawa.

Yuda ataokolewa

Hii inaweza kuweka katika fomu ya kazi. "atamuokoa Yuda kutoka kwa adui zao"

Jeremiah 23:7

Kama Bwana aishivyo

Hili ndilo neno linalotumiwa kwa kiapo.

kutoka nchi ya kaskazini na nchi zote walizofukuzwa

Hii inahusu njia ya makabila kumi ya kaskazini ya Israeli yaliyotumwa na kuenea kati ya nchi zote.

Jeremiah 23:9

Taarifa za jumla

Msemaji amebadilika kutoka kwa Bwana hadi Yeremia.

Kuhusu manabii, moyo wangu umevunjika ndani yangu, na mifupa yangu yote imetetemeka.

Moyo wa nabii umevunjika na mifupa hutetemeka kwa sababu anaogopa hukumu ambayo itatoka kwa uongo wa manabii wa uongo. AT "Nina hofu kubwa nini kitatokea kwa sababu ya manabii wa uongo"

moyo wangu umevunjika ndani

Hisia za nabii zinazungumzwa kama kwamba walikuwa moyo wake. AT "nimesikitika sana"

mifupa yangu yote imetetemeka

Hapa hisia ya hofu inazungumzwa kama kama mifupa ya nabii yalitetemeka. AT "Mimi ninaogopa sana"

Nimekuwa kama mlevi, kama mtu ambaye ameshindwa na divai

Hapa kuna huzuni sana na hofu inazungumzwa kama kama mgonjwa huyo alikuwa kama mtu mlevi. AT "Mimi ni kama mtu mlevi; Siwezi kujidhibiti"

nchi imejaa wazinzi

Kuenea huu hutumiwa kuonyesha kiwango cha dhambi ambacho kilikuwapo wakati wa Yeremia.

wazinzi

Neno hili labda linasimama hapa kwa wazo la kweli ambalo watu wengi katika taifa hilo wamefanya uzinzi dhidi ya wake zao, na pia, kama ilivyo kawaida katika lugha ya kibiblia, kwa wazo la kwamba wamemwacha Bwana ili kuabudu sanamu.

nchi imekauka

Baadhi ya matoleo ya kisasa yanatafsiri maneno haya ya Kiebrania kama "nchi huomboleza."

Jeremiah 23:11

Taarifa ya jumla

Mjumbe hubadilika kutoka Yeremia kwenda kwa Bwana.

makuhani wote wamekufuru

"makuhani ni wenye dhambi"

katika nyumba yangu

Hapa hekalu la Bwana linalinganishwa na nyumba, mahali ambako Bwana anasemekana kuishi kati ya watu wake.

tamko la Bwana

"nini Bwana ametangaza" au "kile Bwana amesema"

kama mahali pa kupumzika katika giza

"si imara, au hatari"

katika mwaka wa adhabu yao

"ikiwa wakati wao wa adhabu unakuja"

Jeremiah 23:13

huenda kwa udanganyifu

"wanaishi katika kutokuwaminifu"

Wanaimarisha mikono ya waovu

"huwaimarisha wale wanaofanya mabaya"

hakuna mtu anarejea na kuacha uovu wake

"Wanaendelea katika dhambi zao"

Wote wamekuwa kama Sodoma....kama Gomora.

"Walikuwa waovu sana"

wormwood was something that was bitter and unpleasant to eat. This phrase describes the punishment that Yahweh was going to bring about on the evil prophets. In the same way, wormwood was bitter and the water was poisonous, so would Yaweh's judgment be on the evil prophets.

Magugu ni kitu kilichokuwa kichungu na kisichofurahisha kula. Maneno haya yanaelezea adhabu ambayo Bwana angeenda kuleta juu ya manabii mabaya. Kwa njia hiyo hiyo, mchanga ulikuwa uchungu na maji yalikuwa yenye sumu, basi hukumu ya Yaweh ingekuwa juu ya manabii waovu.

kufuru imetoka kwa manabii

"Uovu umetoka kwa manabii "

Jeremiah 23:16

Wamekudanganya

"Manabii wamekufanya uamini kitu ambacho si kweli!"

maono kutoka kwenye mawazo yao wenyewe

"maono waliyofikiria"

si kwa kinywa cha Bwana

sio kutoka kwa Bwana

Lakini nani amesimama katika mkutano wa baraza la Bwana? Ni nani anayeona na kusikia neno lake? Ni nani anayezingatia maneno yake na kusikiliza?

Hakuna mtu anayemshauri Bwana. Hakuna mtu anayeelewa kile Bwana anasema. Hakuna mtu anayetii amri za Bwana.

Jeremiah 23:19

dhoruba inazunguka

"ni kama dhoruba kubwa"

Inazunguka vichwa vya waovu

"Inakuja juu ya waovu"

zitakapotimiza nia ya moyo

"Ghadhabu ya Bwana italeta adhabu yote ambayo amepanga"

Jeremiah 23:21

Kwa kuwa kama walisimama katika mkutano wangu wa baraza

"ikiwa wangenisikiliza kweli"

Jeremiah 23:23

Mimi ni Mungu aliye karibu....mimi sio Mungu aliye mbali?

"Mimi ni Mungu ambaye ni wa karibu na mbali."

Je, kuna mtu yeyote anayejificha mahali penye siri ili nisiweze kumwona?

"Hakuna mtu anayeweza kujificha mahali pa siri ili nisiweze kumwona."

Je, sikuijaza Mbingu na Dunia?

"Na mimi niko kila mahali, mbinguni na duniani."

Jeremiah 23:25

Nilikuwa na ndoto!' Je, hii itaendelea mpaka lini, manabii wanaotabiri uongo kutoka kwa akili zao, na wanasema nini kutokana na udanganyifu mioyoni mwao?

"Hii haipaswi kuendelea, manabii wanaotangaza uwongo ambao wao wenyewe wametengeneza."

kuwafanya watu wangu kusahau jina langu..... kwa ajili ya jina la Baali

"kuwaongoza watu wangu wamwabudu Baali badala ya mimi"

Jeremiah 23:28

e, majani yanahusiana na nafaka?

"Majani na nafaka ni vitu viwili tofauti kabisa."

Na neno langu si kama moto? -Hili ni tamko la Bwana-na kama mwamba wenye kupiga nyundo?

"Maneno yangu ni kama moto unaovuna na wenye nguvu," asema Bwana, "na kama nyundo inayovunja mwamba vipande vipande."

kama nyundo inayovunja mwamba vipande vipande

"kama nguvu kama nyundo ambayo inaweza kuponda mwamba"

Jeremiah 23:31

wanaoota ndoto

" ni nani ambao wanadai kuwa na ndoto kutoka kwa Mungu, lakini sio kutoka kwa Mungu.

Jeremiah 23:33

Tamko gani

Swali hili lina maana ya kufanya kazi kama taarifa AT "Hakuna tamko."

Jeremiah 23:35

umepotosha maneno ya Mungu aliye hai

"umebadilisha maneno ya Mungu kusema nini unataka wanasema"

Jeremiah 23:37

Taarifa za jumla

Angalia...

Je, Bwana alisema nini?

"Bwana alisema nini"

Kwa hiyo, angalia

"Kwa hiyo kuwa makini"

nitawachukua na kukutupa mbali na mimi

"Nitawafukuza mbali na mimi"

ambayo haitasahauliwa

"ambayo itaendelea milele"

Jeremiah 24

Jeremiah 24:1

Tazama

Neno "tazama" hapa linaonyesha kwamba Yeremia aliona kitu cha kuvutia.

Maono haya yalitokea......nao Babeli

Sehemu hii ya hadithi hutumiwa kutoa maelezo ya kihistoria kuonyesha wakati matukio yalivyotokea.

mafundi

watu wenye ujuzi wa kutengeneza vitu.

wafua vyuma

watu wenye ujuzi wa kutengeneza vitu kutokana na chuma.

Jeremiah 24:4

neno la Bwana lilikuja

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 1:1.

kama vile tini hizi nzuri

Tini nzuri ni wale waliohamishwa wa Yuda waliotumwa kwenda nchi ya Wakaldayo.

Nitaweka macho yangu kwao wapate mema

"Nitawabariki."

Nitawajenga, wala sitawaangamiza. Nitawapanda, wala sitawang'oa.

Sentensi hizi mbili zina maana sawa. Jambo la pili linaimarisha mawazo ya kwanza. "Nitawasaidia kufanikiwa katika Wakaldayo."

Nitawajenga, wala sitawaangamiza

Neno hili linawafananisha wahamisho na jengo ambalo Bwana atajenga na si kuvunja. AT "Nitawasaidia kufanikiwa katika nchi, na si kuwaangamiza."

Nitawapanda, wala sitawang'oa

"Nitawaweka katika nchi, wala siwaondoe."

hivyo watanirudia kwa moyo wao yote.

"watanirudia kwa uzima wao wote"

Jeremiah 24:8

Lakini kama vile tini mbaya ambazo ni hazifai kuliwa

Maneno haya yanafananisha tini mbaya kwa watu waovu. Tini mbaya ni tini ambazo haziwezi kula na hazifai, watu mbaya hawatamfuata Bwana na pia hawana maana.

Nitawafanya kuwa kitu cha kutisha, wapate maafa

Bwana inalinganisha hukumu ya kuja juu ya watu wa Yerusalemu kwa kitu ambacho kitatisha watu wengine wanapoiona.

Nitatuma upanga, njaa, na tauni dhidi yao

"Nitawaua kwa vita, njaa na magonjwa."

Nitatuma upanga

"Nitawatuma majeshi ya adui"

Jeremiah 25

Jeremiah 25:1

wa nne ... wa kwanza

Angalia

watu wote wa Yuda na wenyeji wote wa Yerusalemu.

Hawa ndio wa mwisho wa Waisraeli. Ufalme wa kaskazini ulikuwa umeanguka tayari.

Jeremiah 25:3

Amoni

(Angalia: tafasili ya majina)

hata leo

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 7:24.

maneno ya Bwana yamekuja kwangu

"Bwana amenipa maneno yake ili kukuhubiri"

Walikuwa na nia ya kwenda nje

"Walikuwa na shauku ya kushiriki maneno ya Mungu na wewe"

kusikiliza au kutega masikio

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 11:6.

Jeremiah 25:5

njia zake mbaya na udhalimu wa matendo yake

Neno "njia mbaya" na "udhalimu wa matendo yake" inamaanisha kitu kimoja na kutaja kila kitu cha dhambi ambacho wanafanya.

kurudi kwenye nchi ambayo Bwana aliitoa wakati wa zamanai kwa ajili ya babu zenu na ninyi, kama zawadi ya kudumu

"ili uweze kurudi nchi ambayo Bwana alikuahidi na kuishi ndani yake milele"

msimkasirishe kwa kazi ya mikono yenu ili kwamba awaumize

"msimfanye Bwana kukasilika kwa kazi zenu za uovu hivyo atakuadhibu"

Jeremiah 25:7

hamkunisikiliza

"hamkunitii"

kuwaleta juu ya nchi hii

Mungu ana mpango wa kutumia Nebukadreza na mikono yake kuwaadhibu Israeli na mataifa ya jirani kwa uasi wao dhidi ya Bwana.

Angalia

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 1:17.

kupiga kelele

Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 18:15

Jeremiah 25:10

mawe ya kusagia

Haya ni mawili makubwa, mawe ya mviringo yanayotumika hupanda nafaka.

Nitafanya mambo haya yote kutoweka kutoka kwa mataifa haya

Haya ni kumbukumbu ya mataifa kuharibiwa.

mataifa haya watamtumikia mfalme wa Babeli

Ulazimishwe kulipa kodi na kuuzwa utumwani.

Jeremiah 25:12

imekamilika

"wakati adhabu yao iko kamili"

kuifanya kuwa ukiwa milele

Mungu ameahidi kuigeuza Babiloni kuwa jangwa kama jangwa.

Nitawalipa kwa matendo yao na kazi za mikono yao

Mungu atawafanya wapate adhabu sawa na waliyoifanya juu ya mataifa waliyoyashinda.

matendo yao na kazi za mikono yao

Maneno haya mawili yanamaanisha jambo sawa na kusisitiza kuwa Yahweh inazungumzia kila kitu ambacho wamefanya kwa mataifa mengine. AT "kila kitu ambacho wamefanya."

Jeremiah 25:15

kikombe hiki cha divai ya ghadhabu kutoka mkononi mwangu, ukawanyweshe mataifa yote niliyokutuma

Bwana anaamuru adhabu kuanza.

ukawanyweshe mataifa yote niliyokutuma

"kufanya mataifa kuwa na uzoefu"

watakunywa na kisha watalewa na kufanya wazimu mbele ya upanga ambao nitaupeleka kati yao

Wale wanaopata matokeo ya adhabu kali ya Bwana watatenda kama watu walichanganyikiwa.

Jeremiah 25:17

Taarifa za jumla

Kifungu hiki kinaendelea mfano wa hasira ya Bwana kama kinywaji kumwagika.

nikawanywesha mataifa yote ambayo Bwana alinituma

Kazi ya kunywa kutoka kikombe cha divai ilikuwa mfano wa hukumu ya Mungu.

kuwafanya kuwa ukiwa na kitu cha kutisha

"kuwaangamiza"

cha kuzomewa na laana

"kupuuzwa au kulaaniwa"

kama ilivyo hata leo

Kulikuwa na kipindi cha muda kati ya wakati hii imeandikwa na wakati ilitokea kweli.

Jeremiah 25:19

Taarifa za jumla

Yeremia anaweka orodha ya mataifa yote ambayo yatahukumiwa

watu wa urithi mchanganyiko

Hii ni kumbukumbu kwa watu wenye wazazi wawili kutoka mataifa mawili tofauti. AT "watu waliochanganywa"

Jeremiah 25:22

Taarifa zajumla

Yeremia anaendelea kuandika mataifa yote yaliyo chini ya hukumu ya Mungu.

Bahari

Hii ni kumbukumbu ya Bahari ya Mediterane.

wale wanyoao nywele zao upande wa pili wa vichwa vya

Hii inawezekana inazungumzia Waarabu ambao waliishi jangwani, watu ambao hukata nywele zao ili waweze kuheshimu mungu wa kipagani.

Jeremiah 25:24

Kunywa

Hii inahusu kikombe cha divai katika maono ya Yeremia ambayo ni mfano wa hukumu ya Mungu.

Zimri

Angalia: tafasiri ya majina

wafalme wa kaskazini

"wafalme kutoka kaskazini"

Jeremiah 25:27

Taarifa za jumla

Maono ambayo Mungu alimpa nabii Yeremia inaendelea.

kunywa na kulewa, kisha tapika, uanguke, wala usisimame mbele ya upanga nitakaoutuma kati yenu

Hii inaonyesha kutokuwepo kwa adhabu ya kuja na ubatili wa kujaribu kuepuka.

kikombe mkononi mwako ili kunywa

"adhabu yao"

lazima mnywe

Hiki si kikombe ambacho mataifa yanaweza kukataa kunywa. Mataifa hawawezi kukataa hukumu za Mungu za vita na majanga ya asili.

kunywa

"kuadhibiwa"

mji unaoitwa na jina langu

"watu wa Yerusalemu"

je ninyi mtaachiliwa msiadhibiwe?

"unapaswa kuadhibiwa."

nitaita upanga juu ya wenyeji wote wa nchi

"Ninawaadhibu wale wanaoishi katika nchi"

Jeremiah 25:30

kuleta mashtaka

"kuwahukumu mataifa" au "kuhukumu na kuadhibu mataifa"

Ataleta haki kwa wote wenye mwili

Mataifa yote inayojulikana atapata hukumu ya Mungu.

wote wenye mwili

"kwa wanadamu wote" au "kwa watu wote"

atawatia waovu katika upanga

"kuwaua watu waovu"

Jeremiah 25:32

Angalia

"Jihadharini na hii!" Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 5:14

dhoruba kubwa itatokea toka pande za mwisho za dunia

"uharibifu unakuja"

watakuja kutoka upande mmoja wa dunia hadi mwingine

"je, siku hiyo itafunika dunia nzima"

Watakuwa kama samadi chini.

Maana iwezekanavyo ni 1) kulikuwa na watu wachache au hakuna watu waliokubali kuzika wale ambao Bwana aliwaua au 2) kulikuwa na ukosefu wa wasiwasi wa miili ya wafu.

Jeremiah 25:34

Wachungaji

Hii ni kumbukumbu kwa viongozi wa Israeli.

Gaagaa katika ardhi

Hii ni ishara ya huzuni, maombolezo au dhiki.

Suku yako

Kwa muda wako" au "wakati wa wewe"

Utaanguka kama kondoo waliochaguliwa.

"Wewe utaangamizwa kwa urahisi"

Mtumwa wa wachungaji waliokwenda

Hakutakuwa na nafasi ya kujificha ili kuepuka hukumu hii au uharibifu.

Yahweh anayaharibu malisho yao

Hukumu ya Mungu ni juu ya viongozi wote na watu, hakuna mtu atakayeokolewa.

Jeremiah 25:37

Hivyo malisho ya amani yataharibiwa

Hapa "malisho" inasimama taifa zima.

yataharibiwa

Hii inaweza kuweka katika fomu ya kazi. AT "ataharibu taifa lote"

ghadhabu ya hasira

Ukweli kwamba Bwana amekasirika husemwa kama kitu. AT "Bwana amekasirika"

Kama simba, ameacha shimo lake, kwa kuwa ardhi yao itakuwa na hofu

Tofauti na marejeo mengine ambako Mungu anaonekana kama simba la kulinda kwa Israeli, katika kifungu hiki Mungu anafanya kama simba ili awaadhibu Israeli. AT "Bwana anakuja kama simba mdogo kuifanya nchi ya watu kuwa hofu"

ardhi yao itakuwa hofu

Hapa "hofu" inasimama ubora. AT "nchi yao itakuwa ya kutisha" au "nchi yao itakuwa kitu cha kutisha kuona"

hasira ya muonevu

Hii inahusu hasira ya maadui wa Israeli.

Jeremiah 26

Jeremiah 26:1

Miji ya Yuda.

"Watu kutoka miji ya Yuda."

Usipunguze neno lolote!

"Usiache kufanya kitu chochote nilichokuambia!"

Ili kwamba nighairi majanga ninayotaka kuyafanya.

Haya ni maelekezo yenye masharti. Kama Yuda watatubu, basi Mungu hatawaangamiza, bali atawaponya.

Jeremiah 26:4

Kama hamtanisikiliza ili mtembee katika sheria yangu ambayo nimeiweka mbele yenu.

"Kama hamtanitii mimi na sheria yangu niliyowapa."

Kisha nitaifanya nyumba hii kuwa kama Shilo.

"Kisha nitaliharibu hekalu."

Nitaifanya nyumba hii kuwa laana.

Hii ni adhabu ya Yahwe ambayo ataileta Yerusalemu.

Katika macho ya mataifa yote juu ya dunia.

"Mataifa yote kwa ajili ya kushuhudia."

Jeremiah 26:7

Nyumba ya Yahwe.

"Hekalu."

Watu wote wakamsimamisha na kusema, "Hakika utakufa!"

Maana zinazowezekana ni 1) Watu waliachagua kuamaini uongo wa amani ya uongo na hawalutaka kukosorewa kwa ukweli 2) Watu waliwaamini manabii wengine wakitangaza amani na kumwona Yeremia kama nabii wa uongo ambaye alistahili kupigwa mawe kwa kuwapotosha watu.

Kwa nini umetabiri kwa jina la Yahwe kwamba nyumba hii itakuwa kama Shilo na mji huu utakuwa ukiwa , bila wakaaji.

Hili ni karipio. "Hupaswi kutabiri katika jina la Yahwe kwamba hekalu lake litaharibiwa."

Jeremiah 26:10

Wakuu.

Mkuu ni mtu mwenye nafasi ya mamlaka.

Lango jipya.

Hili lilikuwa langu mahususi la kuingilia kwenye hekalu.

Mlivyosikia kwa masikio yenu.

"Mmesikia."

Nyumba hii na mji huu.

Watu katika hekalu la Yahwe na mji wa yerusalemu.

Jeremiah 26:13

Kwa hiyo, sasa imarisheni njia zenu na matendo yenu.

Watu walikuwa walikuwa wamejito kumtolea Yahwe sadaka ili kumpendeza. Lakini hawakuwa wanapenda kuifuata sheri ya Yahwe wala kumjua Yeye.

Sikilizenu sauti ya Yahwe.

"Mtiini Yahwe."

Nitendeeni yaliyomema na sahihi katika macho yenu.

Maneno "mema" na "sahihi" yana maana moja.

Kwa ajili ya masikio yenu.

"Kwa ajili yenu kusikia."

Jeremiah 26:16

Si vyema kwa huyu kufa.

Wazee walikili kwamba ujumbe wa Yeremia ulitoka kwa Mungu, nao waliufuata.

Katika jina la Yahwe Mungu wetu.

"Kwa mamlaka ya Yahwe Mungu wetu."

Jeremiah 26:18

Maelezo ya jumla:

Mikaya alikuwa nabii wa Mungu na alifanya huduma ya unabii huko Yuda katika kipindi cha utawala wa Hezekia.

Sayuni utalimwa kama shamba.

"Sayuni utaharibiwa."

Mlima wa hekalu.

Huu ni mlima ambako hekalu lilikuwa limejengwa.

Vichaka.

Neno hili lina maana ya makundi ya vichaka au miti midogo midogo inayokua pamoja karibu karibu.

Je, mfalme Hezekia na watu wote wa Yuda walimua Mikaya?

"Hezekia, mfalme wa Yuda na watu wa Yuda hawakumuua Mikaya."

Je, hakumwogopa Yahwe na kuutaka radhi uso wa Yahwe ili kwamba Yahwe angeghairi kuhusu janga alilotangaza kwao?

Alimwogopa Yahwe na kumfanya Yahwe apunguze hasira ili kwamba Yahwe abadili mtazamo wake kuhusu janga alikuwa amesema atatuma.

Kuutaka radhi uso wa Yahwe.

"Kuifanya hasira ya Yahwe ipungue."

Kwa hiyo tutafanya maovu makubwa juu ya maisha yetu sisi wenyewe?

"Kamaa tutamuua Yeremia, tutaleta uovu mkubwa juu yetu sisi wenyewe."

Jeremiah 26:20

Maelezo ya jumla:

Nabii wa pili, Uria, anathibitisha maneno ya Yeremia.

Katika jina la Yahwe.

Angalia sura ya 26:16.

Wakuu wakasikia maneno yake.

"Wakuu walisikiliza maneno aliyoasema Uria.

Jeremiah 26:22

Maelezo ya jumla:

Uria alikufa kifo cha kinabii katika Yerusalemu.

Maiti.

"Mwili uliokufa."

Mkono wa Ahikamu.

Ahakimu alimsaidia Yeremia na kumlinda.

Elnathani mwana wa Achbori ... Ahikamu mwana wa Shapni.

Haya ni majina ya kiume.

Hivyo hakutiwa mikononi mwa watu ili wamuue.

"Kwa hiyo watu hawakuweza kumuua."

Jeremiah 27

Jeremiah 27:1

Vifungo.

Hiki ni kitu kinachomfunga mtu asitembee au kwenda kwa uhuru.

Kisha akawatuma.

Yeremia ilikuwa atume jozi za vifungo na nira kwa kila mfalme aliyetajwa.

Kwa mkono wa wajumbe hao wa wafalme.

Hapa "mkono" unasimama kuonesha uwakilishi wa hawa wajumbe.

Toa ammri kwao kwa ajili ya mabwana zao.

Yeremia alikjuwa ameelekezwa kutoa jozi za vifungo na nira kwa kila mjumbe na ujumbe ujumbe kwa kila mfalme bila kujali vifungo na nira.

Jeremiah 27:5

Kwa nguvu zangu kuu na mkono wangu ulioinuka.

Kirai "mkono ulionuka" una maana ya nguvu kuu na kina afafanua kiri cha kwanza; "kwa nguvu zangu kuu sana."

Nikawatoa kwa yeyote aliyesahihi katika macho yangu.

"Nampa yeyote ninayetaka kumpa."

Watamtiisha.

Tutakuwa na nguvu na kuwashinda Babeli.

Jeremiah 27:8

Ule usioweka shingo yake chini ya nira ya mfalme.

Wale wasio apa kwa uaminifu kwa mfalme Nebukadreza na kulipa kodi kwa mfalme.

Kwa mkono wake.

Kirai hiki kinamtataja Nebukadreza na majeshi yake.

Hili ni tangazo la Yahwe.

"Hiki ndicho anachosema Yahwe kuwa kitatokea."

Jeremiah 27:9

Maelezo ya jumla:

Yahwe anaendelea kusema na watu wa Yuda kupitia Yeremia.

Watambuzi.

Mtambuzi ni mtu anayefanya utabiri kuhusu mambo yajayo.

Lakini taifa ambalo wataweka shingo zao chini ya nira ya mfalme.

"Lakini taifa watakalomtumikia mfalme."

Hili ni tangazo la Yahwe.

Angalia sura ya 1:7

Watailima.

Hii ina maana ya kuandaa na kutumia ardhi kwa ajili ya kupanda mazao ya chakula.

Kufanya nyumba zao humo.

"Kuifanya Babeli kuwa nyumba yao."

Jeremiah 27:12

Maelezo ya jumla:

Yahwe anaendelea kusema na watu wa Yuda kupitia Yeremia.

Niwekeni shingo zenu chini ya nira ya mfalme wa Babeli.

Mungu anawataka Yuda kumtii na kumtumikia Babeli kama mfalme wao.

Kwa nini mfa-wewe na watu wako-kwa upanga, njaa, na pigo, kama vile nilivyotangaza kuhusu taifa ambalo watapuuza kumtumikia mfalme wa Babeli?

"Utakufa, wewe na watu wako, kwa upanga, njaa, na pigo, kama avile nilivyotangaza kama hamtamtumikia mfalme wa Babeli.

Jeremiah 27:14

Maelezo ya jumla:

Yahwe anaendelea kusema na watu wa Yuda kupitia Yeremia.

Msisikilize maneno.

Yahwe anawaonya watu dhidi ya manabii wa uongo ambao wanawadanganya wakati yeye hata hajawatuma kwao.

Kwa maana mimi sikuwatuma.

"Kwa maanaa mimi sikuwatuma."

Kwa jina langu.

Kirai hiki kina maana ya kuzungumza kwa nguvu za Yahwe na mamlaka au kuzungumza kama mwakilishi wa Yahwe.

Niwafukuze.

"Nowapeleke nje na nchi yenu."

Jeremiah 27:16

Maelezo ya jumla:

Yeremia anaendela kusema neno la Yahwe.

Vyombo vya nyumba ya Yahwe vinarudishwa kutoka Babeli sasa!

Watu kutoka Babeli wanavirudisha vyombo vyote vya dhahabu ambavyo waalivichukua kutoka kwenye hekalu la Yahwe.

Kwa nini mji huu uangamizwe?

"Mji wote utaangamizwa."

Kama ni manabii.

Kama kweli wanachosema ni kweli, basi wangekuwa wanaomba kwamba maneno yangu yasitimie na kwamba vyombo vya hekalu na viongozi wanabaki katika Yerusalemu.

Jeremiah 27:19

Nguzo, bahari, na kitako.

Hivi vilikuwa vifaaa ambavyo vilikuwa hekaluni. "Bahari," lilikuwa beseni la chuma iliyoyeyushwa.

Yehoyakimu.

Maandishi ya Kiebrania yanasema "Yekonia," huu ni utofauti wa jina "Yehoyakimu" ili kuweka wazi kuwa huyu ni mfalme mmoja anayetajwa kwa majina haya.

Jeremiah 27:21

Melezo ya jumla:

Yeremia anaendelea kuzungumza neno la Yahwe.

Hili ni tangazo la Yahwe.

Angalia sura ya 1:7

Jeremiah 28

Jeremiah 28:1

Taarifa za jumla:

Hanania anajidai kuwa anasema ujumbe wa Mungu.

Katika mwaka wa nne na mwaka mwezi wa tano.

Huu ni mwezi wa kalenda ya Kiebrania. Uko katika kipindi cha kiangazi, kati kati ya nusu ya pili ya mwezi Julai na nusu ya kwanza ya mwezi wa Nane katika kalenda ya magharibi.

Azuri

Jina la kiume.

Nimeivunja nira iliyokuwa imewekwa na mfalme wa Babeli.

"Nimestisha mamlaka ya mfalme wa Babeli."

Jeremiah 28:3

Maelezo ya jumla:

Hanania anaendelea kusema.

Hili ni tangazo la Yahwe.

Angalia sura ya 1:7.

Yehoyakimu

Angalia ufafanuzi wa sura ya 27:20.

Jeremiah 28:8

Manabii ambao walikuwepo mbele yangu na mbele yenu

"Manabii walioishi kabla yangu na kabla yenu."

Basi itajulikana kwamba yeye ni nabii kweli aliyetumwa na Yahwe.

"Kisha utajua kweli kwamba yeye ni nabii wa kweli wa Yahwe."

Jeremiah 28:12

Neno la Yahwe likamjia.

Angalia ufafanuzi wa sura ya 1:1.

Ulivunja nira ya mbao, lakini badala yake nitafanya nira ya chuma.

"Mliivunja nira laini lakini sasa nitafanya nira ngumu ambayo hamtaweza akuivunja."

Jeremiah 28:15

Katika mwezzi wa saba.

Huu ni mwezi wa saba katika kalenda ya Kiebrania. uko kati kati ya nusu ya mwisho ya mwezi Septemba na nusu ya kwanza ya mwezi Octoba katika kalenda za Magharibi.

Jeremiah 29

Jeremiah 29:1

Alituma kutoka Yerusalemu.

"Alitangaza kutoka Yerusalemu."

Yehoyakimu.

Maandishi ya Kiebrania "Yekonia," amabayo ni utofauti wa jina "Yehoyakimu." Matoleo mengi ya kisasa yanasema "Yehoyakimu ili kutoa ufafanuzi kwamba anayetajwa ni mfalme yule yule.

Mama yake mfalme.

Hiki ni cheo anachopewa mama wa mfale.

Watumishi wakuu.

Hawa ni viongozi au wakuu muhimu sana.

Elasa mwana wa Shafani na Gemaria mwana wa Hilkia.

Haya ni majina ya kiume.

Jeremiah 29:4

Ambao niliwasababisha.

"Ambaye aliwasababisha" au "ambao Yahwe aliwasababisha."

Jengeni nyumba na musishi ndani yake, pandeni busitani na mle mataunda yake.

Yahwe anawaambia au kuwahakikishia kwamba watakuwemo humo au wataishi humo kwa muda mrefu.

Jeremiah 29:6

Chukueni wake ajili ya wanawenu.

"Waozeni wana wene."

Wapatieni waume binti zenu.

"Waruhusuni binti zenu kuolewa."

Kama mji uko katika amani.

Huu unatajwa mji wa Babeli.

Itafuteni amani ya mji.

Tafuteni kuishi kwa amani na watu wote. Inamaana kwamba wasisababishe shida na kuasi dhidi ya mamlaka.

Jeremiah 29:8

Maelezo ya jumla:

Yahwe anaetelea kusema na mateka wa Isreali.

Tangazo la Yahwe.

Angalia ufafanuzi katika sura ya 1:7.

Jeremiah 29:10

Maelezo ya jumla:

Yaahwe anaendelea kusema yale yatakayotokea kwa Waisraeli mateka.

Ninyi.

Hawa ni Waisraeli ambao ni mateka katika Babeli.

Miaka sabini.

"Miaka 70."

Jeremiah 29:12

Maelezo ya jumla:

Yahwe anaendelea kusema kitakachowapa waisraeli ambao ni mateka huko Babeli.

Mtaniita ... kunioma.

Maneno haya mawili yana maana moja na yanatoa msisitizo kwamba Yahwe atawajibu maombi yao.

Nitawasikiliza.

Hii ina maana kwamba Yahwe atawapa wanachokihitaji.

Nitwarudisha watu wenu waliofungwa.

"Nitayafanya mambo yenu yaende vizuri."

Jeremiah 29:15

Melezo ya jumla:

Yeremia anazungumza na Waisraeli mateka.

Aliyeketi katika kiti cha enzi cha Daudi.

Hapa anatajwa mfalme wa Yuda, ambaye pia ni mmoja wa wazawa wa Daudi.

Ona.

"Angalia" auaa sikiliza" au zingatia."

Niko karibu kutuma upanga, njaa, na ugonjwa juu yao.

"Upanga" unawakilisha vita. "Ninakwenda kuwaadhibu."

Kwa maana nitawafanya kuwa kama tini mbovu ambazo ni mbaya sana hazifai kuliwa.

"Nitawaadhibu kwa ukatili" au nitayaharibu maisha yao."

Jeremiah 29:18

Kushangaza, kitu cha kulaaniwa na kuzomewa, na kitu cha aibu.

Maneno haya yote kwa pamoja yana maana moja na yanaelezea jinsi watu wa mataifa mengine watakavyoitikia watakapoona alichofanya Yahwe kwa watu wa Yuda.

Kulaaniwa na kuzomewa.

Neno "kuzomewa" yana maana aya sauati kubwa za kukataliwa ambayo watu huyasema wanaposema jambo baya kuhusu wengine. Kirai kimsingi kina maana moja na neno kama "laana."

Kusikiliza

"kutii."

Jeremiah 29:20

Kolaya ... Maaseya

Haya ni majina ya kiume.

Ona.

"Angalia" au "sikiliza" au "toa usikivu kwa kilie kinachosemwa."

Niko karibu kuwaweka katika mkono wa Nebukadreza.

"Nitamruhusu Nebukadreza kuwavamia."

Jeremiah 29:22

Laana itatamkwa na wafungwa wote wa Yuda.

Hii inaweza kuandikwa kataika mfumo wa moja kwa moja:"Mateka wa Yuda watasema laana juu watu hawa."

Aliwaoka kwenye moto

"Aliwachoma hadi kufa."

Mimi ndiye nijuaye; mimi ni shahidi

Virai hivi wiwili vina maana moja, na Yahwe anavirudia kwa ajili ya kuweka msisitizo.

Jeremiah 29:24

Shemaya ... Maaseya ... Yehoyada.

Haya ni majina ya kiume.

Mnehelami.

Hili ni jina la kabila la watu.

Kwa jina lako.

"Jina" linamaana ya mamlaka ya mtu na ushuhuda wake. Kwa kuzingatia mamlaka na ushuhuda wako."

Mkatale

Huu ni ubao uliochongwa kwa ajili ya kumuadhibia mtu kwa kushikilia miguu, mikono au kichwa.

Jeremiah 29:27

Maelezo ya jumla:

Hii inamaliza waraka wa Shemaiya ambao aliwatumia watu wa Yerusalemu.

Kwa nini hamkumkemea Yeremia wa Anathothi, ambaye hujifanya mwenyewe nabii nabii juu yenu?

"Mlipaswa kumkemea Yeremia wa Anathothi, ambaye hujifanya mwenyewe nabii huku akisema maneno yalikinyume nanyi."

PJengeni nyummba na musdhinndani yake, na pandeni busitani na kuleni matunda yake.

Angalia ufafanuzi katika sura ya 29:4.

Jeremiah 29:30

Shemaya Mnehelami.

Angalia sura ya 29: 4.

Neno la Yahwe likaja kwa.

Angalia sura aya 1:1.

Tangazo la Yahwe.

Angalia sura ya 1:7.

Jeremiah 30

Jeremiah 30:1

jiandikie mwenyewe katika barua maneno yote niliyotangaza kwako.

"Uandike katika barua ujumbe niliousema kwako."

Maana ona.

"Tazama sikiliza kwa amakini." Hiki ni kiria kinachodai usikivu kwa kile ambacho Yahwe anaenda kukifanya.

Hili ni tangazo la Yahwe.

Angalia ufafanuzi katika sura ya 1:7.

Nitakapowarudisha mateka wa watu wangu.

"Nitafanya mambo yaende vyema kwa watu wangu."

Jeremiah 30:4

Tumesikia.

Neno "tu" lina maana ya Yahwe. Mara kwa mara hujitaja mwenyewe kwa nafisi hii ya wingi, yaani "tu."

Sauti ya kutetemesha na ya hofu na siyo ya amani.

Maana zinazowezakuwa ni 1) Watu walikuwa wakilia kwa sauti kwa sababu hapakuwa na amani" 2) "mnalia kwa sauti ..kwa kuwa hakuna amani."

Jeremiah 30:6

Ulizeni na muone kama mwanaume anazaa mtoto.

"Hakuna mwanaume aliyewahi kujifungua mtoto."

Utakuwa wakati wa huzzuni kwa Yakobo, lakini ataokolewa.

"Kwa vizazi vya Yakobo, lakini nitawaokoa."

Mbona ninamwona kila mwanaume kijana ameshika mikono yake juu ya kiuno chake? Kama mwanamke anayejifungua mtoto, Kwa nini nyuso zao zote zimegeuka rangi?

Yahwe anatumia maswali haya ili kusisitiza jinsi wanaume walivyoogopa. "Bado wanaume vijana wanshikilia vitovu vyao kama mwanamke anayejifungua; wote wanaonekana wagonjwa kwa sababu wameogopa."

Jeremiah 30:8

Maelezo ya jumla:

Yahwe anaendelea kusema kwa Waisraeli.

Nitaivunja nira ya shingo zenu, na Nitaisambaza minyororo yenu.

Maneno haya yote yanaonesha kwamba Yahwe atawaweka huru watu wake wa Israeli dhidi ya utumwa.

Watamwabudu Yahwe.

Neno "wata" linataja watu wa uzao wa Yakobo.

kumtumikia Daudi mfalme wao.

Hapa anatajwa mmoja wa wazawa wa Daudi.

Jeremiah 30:10

Maelezo ya jumla:

Yahwe anaendelea kusema kwa watu wa Israeli.

Mtumishi wangu Yakobo, usiogope ... na usikate tamaa, Israeli.

Virai vyote vina maana moja. Cha pili kinakipa nguvu cha kwanza.

Maana ona.

"Sikilizeni kwa makini."

Na usikate tamaa.

"Na usihuzunike."

Niko karibu kukurudisha kutoka mbali, na uzao wako kutoka nchi ya utumwa.

Virai hivi via maana moja; cha pili kinakipa nguvu cha kwanza.

Kutoka nchi ya utumwa.

"Kutoka sehemu ambako mlikuwa mateka."

Yakobo atarudi.

"Watu watarudi kwenye nchi yao."

Ataokolewa.

"Watu watakuwa salama."

Ambako nimewatawanya.

"Niliko watuma."

lakini hakika sitakuacha.

"Lakini sitakuharibu kabisa kabisa."

Sitakuacha bila kukuadhibu.

"hakika nitakuadhibu."

Jeremiah 30:12

Maelezo ya jumla:

Yeremia ansema ujumbe wa Mungu kwa Waisraeli.

Jeraha lako si lakupona ... kidondda chako ili upone

Hii ina maana akuwa Yahwe amewaadhibu sana na kwamba hakuna mtu wa Kuwasaidia.

Hakuna mtu wa kukutetea kesi yako.

"Hakuna yeyote anayeniomba niwoneshe huruma."

Jeremiah 30:14

Maelezo ya jumla:

Yahwe anaendelea kusema kwa watu wa Israeli.

Wapenzi wako wote.

Yahwe anawaelezea watu wa Israeli kama mke asiyemwaminifu ambaye huchukua wapenzi wengine tofauti na mme wake. Hapa, neno "wapenzi" lina maana ya mataifa mengine. Waisraeli walifanya mapatano nao na kuibudu miungu yao badala ya kumtegemea Yahwe pekee.

Hawatakuangalia.

"Hawataki kuwa arafiki zako tena."

Nimekujeruhi kwa jeraha la adui.

Hii ina maana kwamba Yahwe amewatendea watu wake kama vile anawatendea adui zake.

Kwa nini unaita msaada kwa ajili ya jeraha lako?

Yahwe aliuliza swali hili hapa ili kuwafanya watu wake wajiulize kwa nini wanautafute msaada wake sasa

Dhambi zako zisizohesabika.

"Dhambi zako ambazo ni nyingi sana."

Jeremiah 30:16

Kila mtu akulaye ataliwa, na adui zako wote watend utumwani.

Sentensi hizi mbil zina maana moja. Sentensi ya pili inaimarisha wazo lililosemwa katika sentensi ya kwanza. "Mataifa yote waliowafanya watumwa watafanywa kuwa watumwa."

Kila akulaye ataliwa.

"Wanaowaangamizi ninyi, wataangamizwa na adui zao."

Kwa maana kila aliyekuteka nyara atatekwa, na nitawafanya wote wanaokuwinda kuwa mawindo.

Sentensi hizi mbili zina maana moja. Sentensi ya pili inalipa nguvu wazo la kwanza."Nitawafanya adui za wale walioiba vitu kutoka kwenu katika vita, kuiba vitu kutoka kwao.

Walikuita:Mwenye kutupwa.

Aliyetupwa au aliyetengwa ni mtu ambaye hakubaliwi na watu wengine wala kuruhusiwa kushirikiana na wengine: "waliwaita: 'waliokataliwa au 'walisema, 'hakuna mtu anayekutaka."

Hakuna mtu anayeujali Sayuni.

"Hakuna mtu anayejali kuhusu Sayuni."

Jeremiah 30:18

Taarifa za jumla:

Yahwe anaendelea kusema na watu wa Israeli.

Ona.

"Sikiliza kwa makini."

Niko karibu kuwarudisha mateka wa Hema za Yakobo na kuwa na huruma juu ya nyumba zake.

"Niko karibu kuwafanya uzao wa Yakobo kufanikiwa na nitakuwa na huruma juu yao."

Kisha mji utajengwa juu ya lundo la magofu.

"Kisha wataujenga Yerusalemu juu ya magofu yake"

Kisha wimbo wa kusifu na sauti ya shangwe itasikika kutoka kwao.

"Kisha wataimba wimbo wa kusifu na furaha."

Kwa maana nitawaongeza na wala sitawapunguza.

Virai hivi vyote vinamaana kwamba Mungu ataisababisha idadi ya watu wa Israeli kuongezeka.

Ili kwamba wasifanywe wanyonge.

"Ili kwamba asiwepo mtu wa asiwepo mtu wa kuwashusha."

Jeremiah 30:20

Maelezo ya jumla:

Yahwe anaendelea kuzungumza.

Kusanyiko lao litaanzishwa mbele yangu.

"Nitawaanzisha kama kundi la watu mbele yangu."

Kiongozi wao atatoka miongoni mwao. Atatokeza kutoka kati yao.

Sentensi hizi mbili zina maana moja. sentensi ya pili inaimarisha au kufafanua wazo lililo katika sentensi ya kwanza; "Kiongozi wao atachaguliwa kutoka kwa watu."

Ni nani atakayethubutu kunisogelea?

Yahwe anatumia swali kuweka msisitizo kwamba hakuna mtu mwenye ujasiri wa kumkaribia mpaka Yahwe mwenyewwe amruhusu.

Jeremiah 30:23

Ona, tufni ya Yahwe, ghadhabuyake, imekwenda nje.

Maneno haya yanailinganisha adhabu na ghadhabu au hasira ya Mungu na tufani.Hii inaweka msisitizo kuhusu nguvu na uwezo wake wa kuwaharibu watu waovu.

Jeremiah 31

Jeremiah 31:1

Katika wakati huo

Huu ni wakati ambapo Mungu atawaadhibu waovu.

Hili ni tangazo la Yahwe.

Angalia tafsiri kutoka sura ya 1:7.

Yahwe alinitokea.

Nafsi inayotajwa hapa, "alinitokea", inawakilisha watu wa Israeli.

Jeremiah 31:4

Maelezo ya jumla:

Yahwe anaendelea kusema kwa watu wa Israeli.

Nitakujenga tena kwa hiyo utakuwa umejengwa.

"Nitakufanya imara tena" au nitakufanikisha tena."

Bikra Israeli.

Angalia sura ya 1

Ngoma.

Chombo cha muziki ambacho hutoa sauti kinapopigwa pembeni kwa vipande vya chuma.

Jeremiah 31:7

Sifa zisikike.

"Kila mtu na asikie kusifu kwenu."

Masalia wa Israeli.

"Watu ambao bado hai."

Jeremiah 31:8

Maelezo ya jumla:

Yahwe anaendelea kusema.

Ona.

"Sikilizeni" au "iweni wasikivu."

Kuwaleta.

Neno "kuwaleta" linawataja Waisraeli.

Nitakuwa baba kwa Israeli, na Efraimu atakuwa mzaliwa wangu wa kwanza.

Hapa, "Efraimu" ni jina jingine la "Israeli". 'Nitakuwa kama baba kwa watu wa Israeli, na watakuwa kama mtoto wangu wa kwanza"

Mzaliwa wangu wa kwanza.

Mzaliwa wa kwanza anaheshima na jukumu maalumu.

Jeremiah 31:10

Yule aliyemtawanya Israeli anamkusanya tena.

"Niliwafanya watu wangu kutawanyika kati ya mataifa, lakini nawarudisha nyumbani sasa."

Kama mchungaji alindavyo kondoo zake.

Hii inamaana akuwa Mungu anatunza na kulinda watu wake kama vile mchungaji alindavyo kondoo zake.

Kwa maana Yahwe amemfidia Yakobo na kumkomboa kutoka mkono ambao ulikuwa na nguvu sana kwake.

Virai hivi viwili vina maana ya kitu kimoja, na visisitiza kwamba Yahwe ndiye aliyewaokoa watu wa Israeli: "Maana Yahwe amewaokoa watu wa Israeli dhidi ya adui yao ambaye alikuwa na nguvu sana kuliko wao."

Jeremiah 31:12

Kama busitani iliyomwagiliwa.

Hii ina maana kwamba watakuwa na nguvu na afaya, na watafanikiwa.

Hawatajisikia huzuni tena.

Hii ni inatia mkolozo wa furaha ambavyo watu wa Israeli watakuwa nayo.

Jeremiah 31:13

Nitayageuza.

Hapa, anayetajwa ni Yahwe mwenyewe.

Watu wangu watajijaza wenyewe kwa wema wangu.

"Wema wangu utawaridhisha watu watu wangu."

Jeremiah 31:15

Sauti imesikika katika Rama.

"Nasikia sauti katika Rama."

Ni Raheli akiomboleza kwa ajili ya watoto wake.

Hapa "Raheli" anawakilisha wanawake wa Israeli ambao wanawalilia watoto wao.

Hataki kufarijiwa juu yao, kwa maana hawako hai tena.

"Hatakubali mtu yeyote amfariji, kwa maana watoto wake wamekufa."

Jeremiah 31:16

Kwa nini watu waache kuomboleza?

Yahwe atawarudisha uzao wao kutoka nchi ya adui zao

Jeremiah 31:18

Uliniadhibu, nami nieadhibika.

Kurudiwa kwa maneno haya kunaashiria aidha ukali wa hasira ya Yahwe, au jinsi ilivyo na nguvu hasira yake: "Uliniadhibu sana" au "uliniadhibu, na nimejifunza kutokana na adhabu hiyo."

Nirudishe.

Efraimu anamwomba Mungu ampe moyo wa kufundishika kama ndama asiye na mafunzo.

Niliaibika na kudharirika.

Neno "kuaibika" na "kudharirika" kimsingi yana maana ya moja, na yanaweka mkazo kuhusu swala la kuaibika. "Niliaibika kweli kweli."

Efraimu siyo mtoto wangu wa thamani? Yeye si mpendwa wangu, mwanangu nimpendaye?

"Efraaaimu ni mwanangu wa thamani. Ni mpendwwa wangu, mwanangu nimpedaye.

Jeremiah 31:21

Maelezo ya jumla:

Mungu anaendelea kusema tangu mstari wa saba.

Jiwekee alama za bara bara ... Weka matangazo ... Iweke akili yako ... Rudi.

Virai hivi vimeelekezwa kwa "bikra Israeli."

Iweke akili yako juu ya njia sahihi, njia unayopaswa kufuata.

"Jitahidi sana kukumbuka jinsi ulivyokuja kipindi ulipokuwa umechukuliwa mateka."

Rudi, bikra Israeli!

Mungu anamtaja Israeli aliyebadilika.

Utatanga tanga hadi lini, binti usiyemwaminifu?

Mungu anauliza kuwa mpaka lini watu wake watamuasi."Msisite site kuanza kunitii mimi."

Jeremiah 31:23

Watu.

Hapa hii inawataja watu wa Yuda.

Yahwe akubariki, wewe sehemu takatifu ambapo anaishi, ewe mlima mtakatifu.

Yerusalemu iko juu ya mlima, na hekalu lilijengwa kwenye kilele cha kilima hicho katika Yerusalemu. "Yahwe awabariki wanaoishi pamoja naye katika Yerusalemu, mahali lilipo hekalu lake."

Jeremiah 31:27

Nitakapoipanda nyumba ya Israeli na Yuda na wazawa wa wanadamu na wa wanyama.

"Niwaongeza wanadamu na wanyama kama mkulima apandavyo mazao" au "nitaiiongeza idadi ya wtu na wanyama katika falme za Israeli na Yuda."

Niliwaweka katika uangalizi ili kuwang'oa na kuwabomoa.

"Nilitafuta njia ya kuwang'oa."

Kuwang'oa ... kuwabomoa ... kuwaangusha ... kuwaharibu.

Kung'oa ni kuvuta na kutoa mmea kutoka ardhini; ni kinyume cha kupanda. Kuangusha ni kinyume cha kjenga..Yeremia anatumia maneno haya ambayo karibu yana maana sawa ili kuonesha kuwa kwa hakika mambo haya yatatokea.

Jeremiah 31:31

Angalia.

"Sikiliza" au "toa usikivu kwa kile ninachokwenda kuwaambia."

Hili ni tangazo la Yahwe.

Angalia sura ya 1:7

Jeremiah 31:33

Nitaiweka sheria ya Mungu ndani yao na nitaiandika juu ya mioyo yao.

Virai hivi viwili vina maana moja na vinaweka msisitizo kwamba sheria ya Yahwe itakuwa sehemu yao, kulikio kuwa nayo ikiwa imeandikwa juu ya mawe tu. Hapa "moyo" unawakilisha "hisia" au "akili": Sheria yangu itakuwa sehemu ya mawazo na hisia zao."

Kuanzia mdogo wao hata mkubwa wao.

Kirai hiki kinamaana ya kila mtu, bila kujali umuhimu wao katika jamii.

Jeremiah 31:37

urefu wa mbingu ... misingi ya dunia.

Viraai hivi vina maanisha kwamba uumbaji wote unazungumziwa hapa.

Jeremiah 31:38

Angalia, siku zinauja.

"Zingatia! ambacho nataka kusema kuhusu kitakachotokea hivi karibuni."

Mnara wa Hananeli ... Lango la Pembeni ... Kilima cha Garebu ... Goa ... Bonde la Kidroni ... Lango la Farasi.

Haya ni majina ya shemu mabi mbali.

Litateuliwa.

"Litafanywa takatifu."

Jeremiah 32

Jeremiah 32:1

Neno likaja kwa Yeremia kutoka kwa Yahwe.

"Hiki ndicho alichokisema Yeremia kwa Yahwe."

Alikuwa amefungwa katika uwanja wa walinzi.

"Walimfunga katika uwanja wa walinzi."

Katika uwanja wa walinzi katika nyumba ya mfalme wa Yuda.

Hili lilikuwa eneo la wazi liloungana na ikulu ya mfalme.

Jeremiah 32:3

Kwa nini unatabiri na kusema.

Zakaria anatumia swali kumkemea Yeremia. ("Ni vibaya wewe kuendelea kutabiri na kusema.")

Katika mikono ya mfalme wa Babeli na atauteka

Hapa, "mikono" inamaana ya nguvu au umiliki.

Kwa maana hakika atatiwa.

"Kwa kweli nimeutia mji huu katika mikono ya mfalme wa Babeli.

Mdomo wake utazunguzia kwenye mdomo wa mfalme, na macho yake yatayaona mac ho ya mfalme.

"Sedekia mqenyewe atamuona Nebukadreza ana kwa ana na atazungumza naye."

Hili ni tangazo la Yahwe.

Angalia sura ya 1:7

Unapigana.

Hapa wanatajwa watu wote katika Yerusalemu.

Jeremiah 32:6

Neno la Yahwe likaja kwangu.

Angalia

Hanameli ... Shalumu.

Haya ni majina ya wanaume.

Anathothi

Angalia sura ya 1:1

Jeremiah 32:8

Maelezo ya Jumla:

Yeremia anaendelea kuzungumza.

Shekeli kumi na saba.

"Shekeli kumi na saba." Shekeli 1 ni sawa na gramu 11.

Jeremiah 32:10

Maelezo ya jumla:

Yeremia anaendelea kuzungumza.

Niliandika katika barua na kuitia muhuri, na palikuwa na mashahidi waikaishuhudia.

Hii ni aina ya sahihi ambayo mtu alipaswa kusaini kwa ajili ya kununua ardhi. Watu wengine walipaswa kuwepo kwa ajili ya kushuhudia kwamba nimeinunua adrdhi hiyo.

Kulikuwa na mashahidi wakaishuhudia.

"Palaikuwa na mashahidi ili waone kwamba nimeinunu ardhi hiyo."

Ambayo ilikuwa imepigwa amuhuri.

"Niliyoipiga muhuri."

Baruku ... Neria ... Maaseya.

Haya ni majina ya kiume.

Uwanja wa walinzi.

Angalia ufafanuzi kutoka sura ya 32:1.

Jeremiah 32:13

Maelezo ya jumla:

Yeremia anaendelea kuzungumza.

Mbele yao.

Hapa "yao" anatajwa Hanameli, shahidi, na Wayudea.

Chukua nyaraka hizi, vyote hati hii ya manunuziiliyopigwa muhuri na nakala zisizopigwa muhuri.

"Chukua nyaraka ziliyopingwa muhuri na zile ambazo hazijapigwa muhuri."

Nyumba, mashamba, na mashamba ya mizabibu vitanunuliwa tena katika nchi hii.

"Watu wa Israeli watanunua tena nyumba, bustani za mizabibu na mashamba katika nchi hii."

Jeremiah 32:16

Maelezo ya jumla:

Yeremia anaendelea kuzungumza.

Hati ya manunuzi.

Hii ina maana ya nyaraka au barua iliyotiwa muhuri na ile isiyo tiwa muhuri.

Ole.

"Huzuni"

Kwa nguvu zako kuu na kwa mkono wako ulioinuka.

Kirai "ulioinuka" ni namna ya kuelezea nguvu. Virai hivi viwili kimsingi vina maana moja na vinaelezea ukuu wa Yahwe. "Kwa nguvu zako kuu."

Wewe huonesha agano l uaminifu.

"Unatunza ahadi zako na kuonesha uaminifu wa upendo wako."

Na kumimina makosa ya wanadamu katika mapaja ya watoto wao baada yao.

"Na huwaadhibu watoto kwa sababu ya dhambi za baba zao."

Jeremiah 32:19

Maelezo ya jumla:

Yeremia anaendelea kuzungumza:

Kwa maana amacho yako yanaona njia zote za watu.

"Unaona kila kitu ambacho wanadamu wanafanya."

Ili kumlipa kila mtu stahiki ya matendo yake.

"Na utamlipa kila mtu kulingana matendo na tabia yake"

Ulifanya ishara na maajabu katika nchi ya Misiri.

Haya ni matukio yaliyopita mbapo Mungu alitumia nguvu zake ili kuwatoa utumwani watu wake wa Israeli huko Misiri.

Hata leo.

"Hadi siku ya leo."

Umelifanya jina lako kuwa maarufu.

Hapa "jina" linawakilisha tabia ya Mungu. ("Umejifanya mwenyewe kujulikana.")

Kwa mkono ulioinuka, kwa mkono wenye nguvu.

Virai hivi vyote vinaelezeaa nguvu. Kwa pamoja vinaulezea ukuu wa nguvu za Yahwe. "Kwa nguvu zako kuu."

Jeremiah 32:22

Maelezo ya jumla:

Yeremia anaendelea kuzungumza.

Utawapa.

"utawapa watu wa Israeli."

Nchi itiririkayo maziwa na asali.

Angalia

Lakini hawakuitii sauti yako.

"Lakini hawakutii ulichosema."

Jeremiah 32:24

Maelezo ya ajumla:

Yaremia anaendelea kumwomba Yahwe.

Kuuteka.

"Kwa hiyo jeshi la adu litauteka."

Kwa sababu ya upanga.

Hapa aupanga unamaanisha mapigano ya vita.

Mji umetiwa kwenye mikono ya Wakaldayo.

Hapa "mkono" unamaanisha nguvu au umiliki.

Na mashahidi wameshuhudia.

" Na watu wengine washuhudie jambo hili."

Mji huu unatwa mikononi mwa Wakaldayo.

"Ninautia mji huu mikononi mwa Wakaldayo."

Jeremiah 32:26

Neno la Mungu likaja kwa Yeremia likisema.

"Hiki ndicho alicho Yahwe alimwamabia Yeremia."

Kun kitu chochote kigumu sana kwangu kukifanya?

Yahwe anatumia swali kusisitiza kwamba anaweza kufanya chochote.

Kwenye mikono ya Wakaldayo.

Katika sentensi hii neno "mkono" linawakilisha nguvu au umiliki.

Jeremiah 32:29

Maelezo ya jumla:

yahwe anaendelea kusema kwa Yeremia.

Ili kunikasirisha.

"Kilichonifanya nikasirike sana."

Wanaofanya maovu mbele ya macho yangu.

"Wanaofanya kile ambacho nakihesabu kuwa uovu."

Tangu ujana wao.

"Tangu kipindi walipokuwa taifa."

Matendo ya mikono yao.

"Mambo maovu ambayo wamefanya."

Jeremiah 32:31

Sentensi kiunganishi:

Mstari huu ni mwendelezo wa mistari iliyotangulia.

Mji huu umekuwa sababu ya hasira yangu na gadhabu yangu tangu walipoujenga.

Maneno "hasira" na "gadhabu" kimsingi yana maana moja na yanasisitiza ukuu wa hasira yake Mungu.

Umekuwa hivyo hata leo.

"Wanazidi kunifanya nikasirike hata sasa."

Mbele ya uso wangu.

"Kutoka kwenye uwepo wangu."

Jeremiah 32:33

Maelezo ya jumla:

Yahwe anaendelea kusema kwa Yeremia.

Wamenigeuzia migongo yao badala ya nyuso zao.

"Watu wangu wamenipuuza.

Kupokea marekebisho.

"Hakuna hata mmoja aliyekuwa tayari kujifunza kutoka kwangu."

Watafanya mambo maovu

"Sanamu zao ambazo nazichukia."

Nyumba inayoitwa kwa jina langu.

"Nyumba ambayo ni yangu kabisa."

Bonde la Ben Hinomu.

Angalia

Sikuweka akilini mwangu.

Hapa neno "akilini" linamaanisha mawazo ya Yahwe. Ni kitu ambacho hakuwa kukifiria kuwa watu wake watakifanya, lakini sasa wanakifanya.

Jeremiah 32:36

Ambayo mnasema.

Hapa "mnasema" ni wingi. Maana zilizopo ni 1)Huyu ni Yeremia pamoja na watu alionao, au 2) watu wote.

Umetiwa mikononi mwa mfalme wa Babeli.

Hapa neno "mikono" lina maana ya nguvu au mamlaka. "Kwa hiyo Yahwe ameuweka mji katika mkono wa mfalme wa Babeli."

Kuwakusanya.

"Kuwakusanya watu wanagu."

Jeremiah 32:38

Maelezo ya jumla:

Yahwe anaendelea kusema.

Moyo mmoja na njia moja ya kuniheshimu.

Hii ina maana kwamba kutakuwa na umoja miongoni mwa watu wa Israeli na watamwabudu Yahwe pekee.

Agano la milele.

"Makubaliano ya milele."

Nisiache kufanya mema kwa ajili yao.

"Siku zote nitawafanyia mema."

Ilikwamba wasiniache.

"Ili kwamba siku zote wanitii na kuniabudu."

Jeremiah 32:41

Maelezo ya jumla:

Yahwe anaendelea kusema.

kufanya mema kwwa ajili yao.

Neno "yao", hapa linawataja watu wa Israeli.

Kwa uaminifu nitawapanda katika nchi hii.

"Nitaifanya nchi hii kuwa makazi ya kudumu ya watu wa Israeli."

Kwa moyo wangu wote na maisha yangu yote.

Kwa pamamoja virai hivi viwili vinataja utu kamaili wa mtu.

Jeremiah 32:43

Mashamba yatanunuliwa katika nchi hii.

"Basi watu watanunua mashamba akataika nchi hii."

Mnasema.

Hawa wanaozungumziwa hapa ni watu wa Israeli.

Imetiwa mikononi mwa Wakaldayo.

Hapa "mkono" ni nguvu au umiliki.

Na kuandika katika barua zilizopigwa muhuri.Wtakusanya mshahidi.

Hii ni nyaraka ambayo mtu husaini kwa ajili ya kununua shamba. Watu wengine huwa mashahidi wa ununuzi huo.

Kwa maana nitawarejesha wafungwa wao.

"Kwa maana nitawafanikisha tena."

Jeremiah 33

Jeremiah 33:1

Maelezo ya jumla:

Yahwe anaendelea kujifunua kwa Yeremia kupitia neno lake.

Jeremiah 33:4

Katika hasira na gadhabu yangu.

maneno "hasira" na "gadhabu" kimsingi yana maana moja, na yanaweka msisitizo kuhusu hasira ya Yahwe.

Nitakapouficha uso wangu.

Kirai hiki knaonesha akutoonekana kwa Yahwe katika mji.

Jeremiah 33:6

Nitawarudisha wafungwa.

"Nitayarudisha mafanikio yao."

Jeremiah 33:10

Bila mwanadamu wala mnyama kataika mji huu w Yuda na akatika mitaa ya Yerusalemu ambayo imetengwa bila wakazi, bila mwanadamu wala mnyama.

Mistari hii miwili ina maana amoja na inasisitiza kwamba Yuda imekuwa ukiwa.

Nyumba yangu.

Hekalu katika Yerusalemu.

Wafunwa.

"Mafanikio"

Jeremiah 33:12

Sehemu ya malisho

"Mashamba ya kuchungia makundi yao."

Jeremiah 33:14

Hili ni tangazo la Yahwe.

Angalia sura ya 1: 7

Katika siku hizo na katika wakati huo.

Virai "katika siku hizo" na katika wakati huo" yana maana moja.

Nitachipua shina la haki kwa ajili ya Daudi.

Wazawa wa kiume wa Daudi. "Mtu mwenye haki atatoka katika uzao wa Daudi kama tawi linalostawi kwenye mti.

Nchi.

Taiafa la Israeli.

Jeremiah 33:17

Mtu kutoka Uzao wa Daudi.

"Mtu mwanaume wa uzao wa Mfalme Daudi."

Jeremiah 33:19

Neno la Yahwe lika kwa.

Angalia 1:1

Aganano langu la mchana na usiku ... agano langu na Daudi mtumishi wangu.

Yahwe analilinganisha na mchana na usiku agano lake na Daudi. Kama vile mtu asivyoweza kuubadilisha amchana na usiku, ndivyo pia mtu asivyoweza kulibadilisha agano la Mungu na Daudi.

Kuketi juu ya kiti chake cha enzi.

"Kuutawala ufalme aliopewa."

Kama vile majeshi ya mbinguni yasivyoweza kuhesabika, na kama vile mchanga wa ufukwe wa bahari usivyoweza kupimwa, ndivyo nitakavyouongeza uzao wa Daudi mtumishi wangu na Walawi watumikao mbele zangu.

Sentensi hizi mbili kimsingi zina maana moja na zinaelezea wazo au kitu kimoja. Hivyo zimetumikakwa pamoja ili kuleta msisitizo kuhusu jambo analozungumza Mungu kuhusu Daudi na uzao wake.

Jeremiah 33:23

Neno la Yahwe likaja kwa.

Angalia sura ya 1:1

Hamkuzingatia walichotangaza watu hawa waliposema, "Zile familia mbili ambazo Yahwel alizichagua, sasa amezikataa'?

Swali hilimlimeuizwa kwa lengo la kuweka msisitizo. "Mlipaswa kutambua kuwa watu wanasema kuwa nimezikataa zile koo mbili ambazo nilizichagua."

Jeremiah 33:25

Ni lini Yahwe atawakataa wazao wa Yakobo?

Hatawakataa kamwe

Jeremiah 34

Jeremiah 34:1

Neno lililomjia Yeremia kutoka kwa Yahwe.

"Yahwe alisema neno lake kwa Yeremia."

Wanapigana vita.

"Walikuwa wakipigana."

Na miji yake yote.

Miji inayotajwa hapa ni miji yote jirani na Yerusalemu.

Kuutia mji huu mkono mwa ...

Angalia ufafanuzi kutaka sura ya 32:26.

Mkononi mwa mfalme wa Babel.

Hapa neno "mkono" lina maana ya umiliki. Katika mamlaka ya mfalme wa Babeli."

Hautapona kutoka mkono wake.

"Hautaweza kutoka kwenye mamlaka yake."

Macho yako yatayaangalia macho ya mfalme wa Babeli;atazunguza kwako moja kwa amoja ukiwa aunaenda Babeli.

Maneno haya yote yana maana moja, kwamba atamuona mfalme wa Babeli ana kwa ana.

Jeremiah 34:4

Hautakufa kwa upanga. Utakufa katika amani.

"Hautakufa katika vita, bali utakufa kwa amani.

Hili ni tangazo la Yahwe.

Angalia sura 1:7

Jeremiah 34:6

Lakishi na Azeka.

Haya ni maajina ya miji.

Miji hii ya Yuda ilisalia kama miji yenye ngome.

"Hii ilikuwa miji pekee ya Yuda yenye ngome, ambayo ilikuwa bado haijatekwa."

Jeremiah 34:8

Neno lilomjia Yeremia kutoka kwa Yahwe.

Ujumbe huu hasa hasa unaanzia mstari wa 12 katika sura hii hii.

Neno.

"Ujumbe."

Jeremiah 34:12

Neno la Mungu likaja likaja kwa.

Angaliai

Kila mtu lazima amwachie ndugu yake, Mwebrania mwenzakoaliyejiuza mwewe kwako ili kukutumikia.

"Kila mmoja wenu lazima amwache huru ndugu zake Waebrania ambao walijiuza kwake na kuwa watumwa."

Mwagize aende kwa uhuru.

"Waache wawe huru wasiwe watumishi wako tena."

Hawakunisikiliza wala kutega masikio yao.

Maneno haya yote yanasema kitu kimoja na kimsingi yametumika kwa ajili ya kuleta msisitizo.

Jeremiah 34:15

Yaliyomema katika macho yangu.

"Yalisahihi" au "yanayokubalika."

Kulichafua jina langu.

"Waliacha kufanya mema na kufanya mambo maovu ambayo yamewafanya watu wafikiri kwamba mimi ni mwovu."

Jeremiah 34:17

Kwa hiyo angalia! Niko karibu kutangaza uhuru kwenu ... uhuru wa upanga, tauni, na njaa.

"Kwa hiyo, kwa sababu hamjanitii, nitaruhusu muadhibiwe kwa upanga, tauni, na njaa."

Kwa hiyo angalia.

"Sikiliza" au kuwa makini kusikia kitu muhimu ambacho naenda kukisema."

Walilithibisha mbele zangu.

"Walikubalina nami."

Jeremiah 34:20

Wanaoutafuta uhai wao.

"Wanaotafuta kuwaua."

Hili ni tangazo la Yahwe.

Tangazo la Yahwe ambalo Yahwe ametangaza; au ni kile ambacho yahwe amessema

Ambayo yameinuka dhidi yenu.

"Yamekuja kupigana dhidi yenu."

Na nitawarudisha.

Hapa neno "wao" linamaana ya majeshi ya adui wa taifa la babeli.

Jeremiah 35

Jeremiah 35:1

Warekabi.

Hili ni kabila la watu.

Nyumba yangu

Kirai hiki kinataja hekalu la Yahwe.

Jeremiah 35:3

Yaazania ... Habasinia ... Hanani ... Igdalia ... Maaseya ... Shalumu.

Haya ni majina ya Yahwe.

Jeremiah 35:5

Warekabi.

Angalia ufafanuzi katika mstari wa kwanza wa sura hii ya 35.

Yonadabu ... Rekabu.

Haya ni majina ya kiume.

Ili kwamba muweze kuishi miaka mingi katika nchi.

Neno "Siku" , hapa linamaanisha kipindi cha maisha kirefu."

Jeremiah 35:8

Sauti ya Yonadabu.

Neno "sauti" hapa linamaana ya "amri". (Amri ya Yonadanu.")

Siku zetu zote.

Neno "siku", hapa lina maana ya kipindi kirefu cha maisha."

Jeremiah 35:12

Neno la Yahwe likaja kwa.

Nii ni namna ya kuweka utangulizi wa kile anachokwenda kusema Yahwe

Hamgtapokea maelekezo na kusikiliza neno langu?

Swali hili limeulizwa kwa ajili ya kuwakemea Israeli.

Yonadabu ... Rekabu.

Haya ni majina ya kiume.

Maneno ya Yonadabu mwana wa Rekabu aliyowapa wanawe kama amfri, wasinywe divai yoyote, yameheshimiwa.

Wana wa Yonadabu, wana wa Rekabu, waliishika amri ya baba yao ya kutokunywa divai."

Jeremiah 35:15

Kila mtu aache uovu wake na kutenda matendo mema.

Maneno haya yote yana maana moja na yameunganishwa kwa ajili ya kuweka mkazo.

Kuifuata miungu mingine na tena kuiabudu.

Maneno haya yanamaanisha kitu kimoja, yameunganishwa pamoja kwa ajili ya kuweka mkazo.

Bado hamtanisikiliza wala kutegaa masikio yenu kwangu.

Maneno haya yana maana moja na yameunganishwa kwa ajili ya kuweka mkazo au msisitizo.

Jeremiah 35:17

Angalia.

Neno hili linatuandaa akutega masikio kwa makini ili kusikia jambo linaloenda kusemwa.

Jeremiah 35:18

Warekabi.

Hili ni jina la kabila la watu. Angalia ufafanuzi katika mstari wa kwanza katika sura hii ya 35.

Yonadabu ... Rekabu.

Haya ni majina ya kiume. Pia angalia mstari wa kwanza katika sura hii ya 35.

Jeremiah 36

Jeremiah 36:1

Taarifa ya jumla:

Tazama: uandishi wa shairi.

Ikawa

"ikatokea" Neno hili limetumika kuonesha kuwa ni mwanzo wa simulizi mpya.

Katika mwaka wa nne wa Yehoyakimu mwana wa Yosia mfalme wa Yuda

Tazama namna ulivyotafsiri katika sura ya 25:1

Kuwa neno hili

"neno hili"inaonesha ujumbe unaofuata.

Kila taifa

"mataifa yote"

Nimekwambia toka

"nimekwambia wewe toka"

Tangu siku za Yosia mpaka leo

"toka siku za Yosia mpaka leo"

Yamkini watu wa Yuda

"Labda watu wa Yuda"

Nimedhamiria kuwafanyia

"Nimepanga kuwafanyia"

Labda kila mtu

"ili kila mtu"

Toka kwenye njia yake ya uovu

"toka kwenye uovu wake"

Jeremiah 36:4

Baruku akaandika katika kitabu toka kwenye maneno aliyosomewa na Yeremia, maneno yote aliyoyasema Bwana kwake

"Yeremia alipokuwa akizungumza, Baruku aliandika maneno yote ambayo Bwana aliyazungumza kwa Yeremia"

Soma toka kwenye kitabu

"soma kwa nguvu toka kwenye kitabu"

kama ninavyokusomea

"kutokana na ninayoyasema"

lazima usome

"lazima usome kwa nguvu"

katika masikio ya watu wa nyumba yake

"Ili watu wa nyumba ya Bwana wasikie"

kwenye masikio ya Yuda wote waliokuja toka kwenye miji yao

"ili watu wote wa Yuda waliokuja toka kwenye miji yao wasikie"

Jeremiah 36:7

Taarifa ya jumla:

Yeremia anaendelea kumpa maelekezo Baruku.

Yamkini

"labda"

Wao wataomba rehema

"wao" inawakilisha watu wa nyumba ya Bwana na nyumba ya Yuda waliokuja katika nyumba ya Bwana toka kwenye miji yao.

wataomba rehema mbele za Bwana

"Bwana atasikiliza maombi yao ya Rehema"

Labda kila mtu ataacha njia yake mbaya

"Labda watatubu; kila mtu ataacha njia yake mbaya"

Njia yake mbaya

"njia yake mbaya"

Ghadhabu na hasira

"hasira"

Jeremiah 36:9

Ikawa

"ikatokea" Neno hili limetumika kuonesha kuwa ni mwanzo wa simulizi mpya.

katika mwaka wa tano na mwezi wa tisa

Huu ni mwezi wa tisa wa kalenda ya Kiebrania. Ni katika kipindi cha mwisho cha Novemba na mwanzo wa Disemba kwa kalenda ya Mashariki.

Yehoyakimu mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda

Tazama ulivyotafsiri katika sura ya 25:1

kutangaza mfungo

"kutoa wito kwa kila mtu kushiriki katika mfungo"

Gemaria mwana wa Shafani

Haya ni majina ya watu.

mwandishi

"aliyekuwa mwandishi"

katika lango la kuingilia nyumbani mwa Bwana

"katika lango jipya la kuingilia katika nyumba ya Bwana"

Alifanya hivi

Alisoma kwa nguvu maneno ya Yeremia.

katika masikio ya

"katika masikio ya Yerusalemu"

Jeremiah 36:11

Mikaya

Hili ni jina la mtu.

Mikaya mwana ya Gemaria mwana wa Shafani

"Mikaya ambaye ni mwana wa Gemaria, ambaye ni mwana wa Shafani"

Chumba cha karani

"chumba cha mwandishi"

Tazama

"tazama" inaongeza msisitizo kwenye jambo linalofuata.

Elishama ... Delaya

Haya ni majina ya watu.

Shemaya

Hili ni jina la mtu.

Elnathan mwana wa Akbori

Elnathani mtoto wa Akbori

Gemaria mwana wa Shafani

"Gemaria mtoto wa Shafari"

Sedekia

Hili ni jina la mtu.

Hanania

Hili ni jina la mtu.

Na wakuu wote

"na wakuu wengine wote"

Jeremiah 36:13

Mikaya

Hili ni jina la mtu.

Akawasili kwao

Neno "kwao" linamaanisha wakuu.

kwenye masikio ya watu

"ili watu wasikie"

Yehudi ... Nethania ... Shelemia ... Kushi

Haya ni majina ya watu.

soma kitabu

"soma kitabu kwa nguvu"

Jeremiah 36:16

Ikatokea kwamba

Maneno haya yanaonesha umuhimu wa tukio katika simulizi.

Wao waliposikia

Neno "wao" linamaanisha wakuu.

Maneno haya yote

maneno yote ambayo Baruku aliyasoma kwa nguvu toka kwenye kitabu.

Uliyaandikaje

"uliyaandika kwa namna gani"

Aliyosomewa na Yeremia

"Yeremia alipokuwa akizungumza, Baruku aliandika maneno yote ambayo Bwana aliyazungumza kwa Yeremia"

Kusema

Yeremia alizungumza kwa nguvu ili Baruku aandike maneno yake.

kuyaandika na wino

"alitumia wino kuandika"

wino

Wino mweusi unaotumika kuandikia

Na Yeremia pia

"Yeremia pia anatakiwa ajifiche."

Mko wapi

Maneno haya yanawaelezea Baruku na Yeremia.

Jeremiah 36:20

Kisha wao

Neno "wao" linawaelezea wakuu.

Wakakiweka kitabu katika chumba cha Elishama

"wakakiweka kitabu sehemu salama katika chumba cha Elishama"

Elishama karani

"Elishama aliyekuwa mwandishi"

Maneno haya

Maneno ya kwenye kitabu ambayo Yeremia alimsomea Baruku.

Yehudi

Hili ni jina la mtu.

katika mwezi wa tisa

Huu ni mwezi wa tisa kwa kalenda ya Kiebrania. Majira haya ni mwishoni mwa msimu wa kupanda na mwanzo wa kipindi cha baridi.

Na mkaa ulikuwa ukiwaka mbele yake

"Na mkaa ulikuwa mbele yake ukiwa unawaka"

Makaa

Ni sehemu ya moto ambayo mtu anaweza kuihamisha

Jeremiah 36:23

Ikatokea kwamba

Maneno haya yanaonesha umuhimu wa tukio katoka simulizi.

Yehudi

Hili ni jina la mtu.

Kurasa

Hizi ni kurasa za maneno katika kitabu.

itakatwa

"ile sehemu itakatwa"

na kisu

"kwa kutumia kisu cha mwandishi"

Makaa

Ni sehemu ya moto ambayo mtu anaweza kuihamisha

Mpaka kitabu chote kilipoharibiwa

"mpaka kitabu kilipokwisha kabisa"

maneno haya yote

Maneno toka kwenye kitabu ambacho Baruku alikiandika kwa kusomewa na Yeremia.

wakararua mavazi yao

Watu huchana mavazi yao wakiwa na huzuni sana.

Jeremiah 36:25

Elinathani ... Delaya na Gemaria

Haya ni majina ya watu.

Wakamsihi mfalme

"Wakamuomba mfalme"

Yerameeli ... Seraya ... Azrieli ... Shelemia ... Abdeeli

Haya ni majina ya watu.

ndugu

"ndugu wa mfalme"

Jeremiah 36:27

Neno la Bwana lilikuja

"Bwana alizungumza neno lake"

Kwa maneno ya Yeremia

"Yeremia alipokuwa akizungumza, Baruku aliandika maneno yote ambayo Bwana aliyazungumza kwa Yeremia"

Rudi, ukachukue kitabu kingine mwenyewe

"chukua kitabu kingine tena mwenyewe"

Kitabu cha awali

"kitabu cha kwanza"

Kwa nini umeandika juu yake

Yehoyakimu alitumia swali ili kusisitiza kuwa Yeremia hakupaswa kuandika kuwa mfalme wa Babeli atakuja na kuvamia.

kwa kuwa ataharibu

"na ataharibu"

Jeremiah 36:30

Hatakaa katika ufalme wa Daudu

"hatatawala kama mrithi wa Daudi"

Maiti yako itatupwa nje

"watu wataitupa maiti yako nje"

maiti yako

"mwili wako uliokufa"

kwenye siku ya jua

"ili itolewe katika siku yenye joto"

ninyi nyote

"ninyi nyote"

Jeremiah 36:32

Maneno ya Yeremia

"Yeremia alipokuwa akizungumza, Baruku aliandika maneno yote ambayo Bwana aliyazungumza kwa Yeremia"

Kilichochomwa moto na Yehoyakimu mfalme wa Yuda

"Ambacho Yehoyakimu mfalme wa Yuda alikichoma kwa moto"

Hatahivyo, maneno mengine yaliyofanana yaliongezwa katika kitabu hiki

"Hatahivyo Yeremia na Baruku waliongeza maneno mengi yaliyofanana na maneno yaliyokuwa kwenye kitabu cha mwanzo."

Jeremiah 37

Jeremiah 37:1

Yehoyakimu

Katika maneno ya Kiebrania wana Konia.

wa nchi

"wa nchi ya Yuda"

Alitangaza

"Bwana alitangaza"

Kwa mkono wa nabii Yeremia

"kupitia Yeremia ambaye ni nabii."

Jeremiah 37:3

Yehukali

Hili ni jina la mtu.

Shelemia

Hili ni jina la mtu.

Sefania mwana wa Maaseya the Prist

Sefania mwana wa Maaseya aliyekuwa kuhani.

kwa niaba yetu

"kwa ajili yetu" Neno "yetu" linamuelezea mfalme Sedekia na watu wote wa Yuda.

Yeremia alikwenda na kutoka kati ya watu

"Yeremia aliweza kwenda kokote alipotaka na mtu yeyote"

Kwa kuwa hajawahi kuwekwa gerezani

"Kwa sababu hakuna mtu aliyemuweka gerezani"

kuja nje

"kuitoa nje"

Kuzingatia

Tazama ulivyotafsiri katika sura ya 32:1

Jeremiah 37:6

Neno la Bwana lilikuja

Bwana alizungumza neno lake

mtasema

Maneno haya yanazungumzwa na watu wawili ambao mfalme Sedekia aliwatuma kwa Yeremia.

Kuomba ushauri kwangu

Neno "kwangu" linamuelezea Bwana.

Tazama

Neno hili linaongeza msisitizo wa ktu kinachofuata.

Watapigana dhidi ya mji huu, wataukamata na kuuchoma moto.

"kupanga vita dhidi yao, kuuchukua na kuuchoma moto"

Jeremiah 37:9

Msijidanganye wenyewe

Neno "wenyewe" linawaelezea mfalme Sedekia na watu wote wa Yuda.

Hakika Wakaldayo wanatuacha

Watu wa Yuda wanafikiri kuwa watakuwa salama kwa sababu Wakaldayo wameondoka.

watainuka

"watu waliojeruhiwa watainuka"

Jeremiah 37:11

Ilikuwa

"Ikawa" Neno hili lilitumika kuonesha mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

Eneo la nchi

"sehemu ya nchi"

Kati ya watu wake

"kati ya ndugu zake" Yeremia alikua anatoka katika mji wa Anasosi katika nchi ya Benyamini.

Lango la Benyamini

Hili ni jina la mlango.

Yeria

Hili ni jina la mtu

Shelemia

Hili ni jina la mtu

Hanania

Hili ni jina la mtu.

Kuhamia kwa Wakaldayo

"Kukimbilia kwa Wakaldayo"

Jeremiah 37:14

Hiyo sio kweli

"Huo ni uongo"

kutohamina

"kutokukimbia"

Yeria

Hili ni jina la mtu.

Wakuu

Tazama ulivyotafsiri katika sura ya 1:17

Walikuwa na hasira

"walikuwa na hasira sana"

Yonathani mwandishi

"Yonathani aliyekuwa mwandishi"

Jeremiah 37:16

Yeremia aliwekwa katika gereza la chini

"wakuu walimuweka Yeremia katika chumba kilichokuwa chini"

wakamleta

"wakamleta Yeremia"

nyumba yake

"nyumba ya kifalme ya mfalme Sedekia"

utapewa

Maneno haya ni kwa ajili ya mfalme Sedekia na watu wake.

Kutiwa katika mikono ya mfalme wa Babeli.

Tazama ulivyotafsiri katika sura ya 32:3

Jeremiah 37:18

Namna nilivyofanya dhambi dhidi yako ... gerezani?

Yeremia alitumia swali kusisitiza kuwa hakufanya kosa lolote.

watu hawa

Watu wa ufalme wa Yuda

wameweka

"wameweka"

wako wapi manabii wako, waliokutolea unabii... dhidi ya nchi hii

Yeremia alitumia swali ili kusisitiza kuwa manabii wengine walikuwa waongo lakini yeye hakufanya kosa lolote kwa sababu aliwaambia ukweli.

Manabii wenu

Maneno haya yanaelekezwa kwa mfalme Sedekia na watu wa ufalme wa Yuda.

Hatakuja dhidi yako wala nchi hii

"hatakuvamia wewe wala nchi hii"

ombi langu limekuja mbele yako

Linganisha na namna ulivyotafsiri katika sura ya 36:7 "maombi yao ya rehema yakafika mbele za Bwana"

Nyumba ya Yonathani mwandishi.

Nyumba ya Yonathani aliyekuwa mwamndishi.

Jeremiah 37:21

ya walinzi

"ya watu waliokuwa wakilinda"

Alipewa mkate

"Mtumishi wake alimpa Yeremia mkate"

Toka kwenye mtaa wa waokaji

"toka kwenye mtaa ambao waokaji wanafanya kazi"

Jeremiah 38

Jeremiah 38:1

Shefatia ... Malkiya

Majina ya kwenye orodha hii ni majina ya wanaume.

watauawa kwa upanga, njaa na tauni

"watakufa kwa upanga, njaa na tauni"

Atakimbia kunusuru maisha yake

Waliojisalimisha Babeli watakimbia kuyanusuru maisha yao htakama watapoteza mali zao.

Mji huu utatiwa mikononi mwa jeshi la mfalme wa Babeli

"nitaliruhusu jeshi la mfalme wa Babeli kuiteka Yerusalemu"

ataikamata

"jeshi lake litaikamata"

Jeremiah 38:4

Atafanya mikono ya wapiganaji waliobaki mjini kuwa dhaifu, ma mikono ya watu wote

"atasababisha askari na watu wa mji kupotezaujasiri"

Kwa kuwa mtu huyu hawapi usalama watu hawa bali maafa

"kwa sababu Yeremia hawasaidii watu bali anawaumiza watu"

Tazama yuko mikononi mwenu

"Tazama, mna nguvu juu yake"

Jeremiah 38:6

Mtupeni katika birika

Birika ni sehemu iliyochimbwa chini ya ardhi inayotumika kuhifadhia maji ya mvua.

Wakamshusha chini Yeremia kwa kutumia kamba

Hii inaelleza namna walivyomtupa Yeremia katika shimo.

Jeremiah 38:7

Ebedi Meleki Mkushi

Hili ni jina la mtu kutoka Kushi.

Sasa mfalme

Neno "sasa" linasimamisha simulizi na mwandishi anatuelezea historia ya alichokua akikifanya mfalme.

Kukaa katika lango la Benyamini

Sedekia alikuwa akisikiliza na kuamua keshi za jinai.

Lango la Benyamini

Hili ni lango la kuingilia Yerusalemu ambapo watu waliliita Benyamini mwana wa Yakobo.

Jeremiah 38:10

Watu thelathini

"watu 30"

walitumia kamba kushuka chini

"walitumia kamba kushuka chini"

Jeremiah 38:12

na juu ya kamba

"na kuzunguka kamba"

Walimvuta Yeremia

Hawa ni baadhi ya watu thelathini waliokuwa na Ebedi Meleki.

Jeremiah 38:14

Ikiwa nitakujibu, je hautaniua?

Yeremia alitumia swali kuonesha uhakika wake kuwa mfalme atamuua endapo atasema ukweli.

Kama Bwana aishivyo, yeye aliyetuumba

Mfalme alizungumza haya ili kuonesha kuwa anayokwenda kuyasema ni kweli.

Mimi sita ... kutia katika mikono ya watu hawa

"mikono" inamaanisha nguvu ya kutawala. "Sitawaruhusu ... watu hawa kukukamata"

wanatafuta maisha yako

"wanajaribu kukuua"

Jeremiah 38:17

Mungu wa Israeli

"Mungu wa wana wa Israeli"

Mji huu hautachomwa moto

"jeshi la Babeli halitachoma moto mji huu"

mji huu utatiwa mikononi mwa Wakaldayo

"Nitaruhusu Wakaldayo wauteke mji huu"

Hamtakimbia toka kwenye mikono yao

"hamtakimbia toka kwenye nguvu yao"

Jeremiah 38:19

Nitawatia katika mikono yao

Hapa neno "mkono" linamaanisha "nguvu" au "utawala"

kwa wao kunitendea vibaya

Neno "wao" linamaanisha Watu wa Yuda.

Jeremiah 38:20

Hawatakutia kutika mikono yao

Wakaldayo hawatakutia katika mikono ya Yuda.

Hivi ndivyo alivyonionesha Bwana

Neno "hivi" linaonesha maneno ambayo Yeremia atayasema baadae.

Jeremiah 38:22

Taarifa ya Jumla:

Yeremia anaendelea kuongea na mfalme Sedekia.

Wanawake wote waliosalia ... watatolewa nje kwa wakuu wa mfalme wa Babeli

"askari watawatoa nje wanawake wote waliosalia ... nje kwa wakuu wa mfalme wa Babeli"

Umedanganywa na rafiki zako

"Rafiki zako wamekudanganya"

Miguu yako inazama katika matope

Hii inamaanisha kuwa mfalme yupo katika wakati mgumu.

Kwa kuwa wake zako na watoto wako wateletwa nje kwa Wakaldayo

"Askari watawaleta wake zako na watoto wako nje kwa Wakaldayo"

Hawatakimbia toka katika nchi yao

"hawatakimbia toka kwenye utawala wao"

Utakamatwa kwa mkono wa mfalme wa Babeli, na mji huu utachomwa moto.

"Jeshi la mfalme wa Babeli litakukamata na kuuchoma moto mji.

Jeremiah 38:24

Yonathani

Hili ni jina la mtu.

Jeremiah 38:27

Mpaka siku Yerusalemu ilipokamatwa

"mpaka siku ambayo jeshi Babeli liliikamata Yerusalemu.

Jeremiah 39

Jeremiah 39:1

Katika mwaka wa tisa mwezi wa kumi wa Sedekia mfalme wa Yuda

Huu ni mwaka wa kumi kwa kalenda ya Kiebrania. Ni mwishoni mwa mwezi wa Disemba na mwanzoni mwa mwezi wa Januari katika kalenda ya mashariki.

tisa ... kumi ... kumi na moja ... nne

tisa ... kumi ... kumi na moja ... nne

Katika mwaka wa kumi na moja mwezi wa nne wa Sedekia, siku ya tisa ya mwezi

Huu ni mwezi wa nne kwa Kalenda ya Kiebrania.

Nergal-Shareza, Samgari, Nebo na Sasechimu

Haya ni majina ya watu.

katika lango la katikati

"Katikati ya lango la kuingilia mjini" Ilikuwa ni kawaida kwa viongozi kukaa katika lango la mji na kujadili mambo mbalimbali.

Jeremiah 39:4

Wakaenda nje usiku toka mjini kwa njia ya bustani ya mfalme

"waliondoka mjini usiku wakaenda kupitia njia ya bustani ya mfalme"

Nchi tambarare ya Yeriko

Hii ni nchi iliyo tambarare iliyoko kusini mwa bonde.

Ribla katika nchi ya Hamathi

Ribla ulikuwa mji katika himaya ya Hamathi.

wakawafuata na kuwapata

"wakawafuata na kuwakamata"

Wakatoa hukumu juu yake

"wakaamua namna ya kumuhukumu"

Jeremiah 39:6

Mbele ya macho yake

"alipokuwa akitazama"

Aling'oa macho ya Sedekia

"watu wa mfalme walimpofusha Sedekia"

Jeremiah 39:8

Nebuzaradani

Hili ni jina la mwanaume.

Walinzi wa mfalme

"wanaomlinda mfalme"

Watu wengine waliobakia mjini

"watu waliosalia katika mji"

Jeremiah 39:11

Nebuzaradani ... Gedalia ... Ahikamu ... Shafani

Haya ni majina ya watu.

kuwatuma watu

"kuwatuma watu kwenda kumchukua Yeremia"

Kati ya watu

"kati ya watu waliosalia Yuda"

Jeremiah 39:15

Taarifa ya jumla:

Simulizi hii ilitokea kabla ya matukio ya mwanzoni.

Sasa

Hii inaonesha mwanzo wa simulizi.

neno la Bwana lilimjia Yeremia ... akasema

"Bwana akazungumza na Yeremia. Akisema"

Ebedi Meleki Mkushi

Ebedi Meleki mtu wa nchi ya Kushi.

Ninakaribia kutimiza maneno yangu juu ya mji huu sio kwa kuangamiza na sio kwa wema

"nitaleta maafa juu ya mji huu kama nilivyosema kuwa nitafanya"

Na yote yatakuwa kweli mbele yako siku hiyo

"kwa kuwa utayaona yakitokea siku hiyo"

Jeremiah 39:17

Taarifa ya jumla:

Bwana anaendelea kuongea na Yeremia.

Siku hiyo

Hii ni siku ambayo watu wa Babeli watabomoa ukuta wa Yerusalemu na kuuharibu mji.

Asema Bwana

"aliyoyasema Bwana"

Hamtatiwa katika mikono ya watu mnaowaogopa

"Watu mnaowaogopa hawatawadhuru"

Hamtaanguka kwa upanga

"hakuna atakayewaua kwa upanga"

Mtakimbia na kuponya maisha yenu ikiwa mtaniamini

"kwa sababu ya kuniamini mimi hamtauawa"

Jeremiah 40

Jeremiah 40:1

Haya ni maneno yaliyokuja kwa Yeremia toka kwa Bwana

"haya ndiyo aliyoyasema Bwana kwa Yeremia"

Nebuzaradani, kiongozi wa askari wa mfalme

Nebuzaradani aliyekuwa kiongozi wa askari wa mfalme.

Hapo ndiko alikopelekwa Yeremia na alipokuwa amefungwa minyororo

"Hapo ndipo askari wa Babeli walipompeleka Yeremia na kumfunga minyororo"

waliotakiwa kupelekwa uhamishoni Babeli

"ambao askari waliwatuma Babeli"

Jeremiah 40:3

Bwana alikuja. na akafanya kama alivyosema

"Bwana alifanya kama alivyowaambia kuwa atafanya"

Kwa kuwa mmeasi mbele yake na hamkusikiliza sauti yake

"Kwa kuwa ninyi Yuda mmefanya dhambi juu ya Bwana na hamkusikiliza amri yake"

jambo hili limetokea

"uharibifu umetokea"

Basi tazama

Nebuzaradani alisema haya ili kumfanya Yeremia awe makini kumsikiliza kwa wakati huo.

ni njema machoni pako

"unayotaka"

Jeremiah 40:5

Gedalia ... Ahikamu ... Shafani

Haya ni majina ya watu

Kati ya watu

"kati ya Wayahudi"

Ni njema machoni pako

"unayofikiri ni nzuri"

Waliosalia katika nchi

"waliobaki Yuda"

Jeremiah 40:7

Sasa

Hii inaonesha kuwa ni mwanzo wa simulizi.

wale ambao hawakwenda uhamishoni Babeli

"wale ambao maadui hawakuwapeleka Babeli"

Ishmaeli ... na Yezania

Haya ni majina ya watu.

mwana wa Mmaaka

Huyu ni mtu wa dini ya Maka.

Jeremiah 40:9

akawaapia

"akaapa kwa makamanda wa yuda"

matunda ya wakati wa jua

Haya ni matunda ya msimu.

Kaeni katika miji yenu

"kaeni katika miji yenu"

Jeremiah 40:11

Wayahudi wote

Watu wote wa Yuda

Kati ya watu wa

"watu wote wa Yuda kati ya watu wa Amoni."

mabaki ya Yuda

"mabaki ya watu wa Yuda"

alimchagua ... juu yao

"alimuweka ... kuwa juu yao"

Gedalia mwana wa Ahikamu mwana wa Shafani

Haya ni majina ya watu.

juu yao

"juu ya watu wa Yuda"

ambako wametawanywa

"ambako Babeli waliwapeleka"

divai na matunda ya jua kwa wingi

"kiasi kikubwa cha zabibu na matunda ya jua"

matunda ya jua

Matunda ya msimu.

Jeremiah 40:13

Yohana ... Karea

Haya ni majina ya watu.

Gedalia

Hili ni jina la mtu.

Unafahamu kuwa mfalme Baalisi wa watu wa Amoni alimtuma Ishamaeli Mwana wa Nethania akuue?

"unapaswa kufahamu kuwa Baalisi Mfalme wa watu wa Amoni alimtuma Ishmaeli mwana wa Nethania ili akuue"

Baalisi

Hili ni jina la Mfalme

Ishmaeli mwana wa Nethania

Haya ni majina ya watu.

Ahikamu

Hili ni jina la mtu.

Jeremiah 40:15

Yohana ... Karea

Haya ni majina ya watu.

Kuongea na Gedalia pembeni

"kuongea na Gedalia kwa siri"

Gedalia

Hili ni jina la mtu.

Ishmaeli mwana wa Nethania

Haya ni majina ya watu.

Hakuna atakayenihisi mimi

"hakuna atakayejua"

Kwa nini akuue wewe

"usimruhusu akuue"

Kwa nini uruhusu Yuda wote

"Usiruhusu watu wengi wa Yuda"

Yuda wote waliokusanyika kwako

"watu wa Yuda waliokuja kwako"

kutawanyika

"kwenda mbali kwenye nchi tofauti"

Na waliosalia Yuda wataharibiwa

"na kuruhusu watu wa Yuda waharibiwe"

masalia wa Yuda

"waliosalia Yuda"

Ahikamu

Hili ni jina la mtu.

Jeremiah 41

Jeremiah 41:1

Ikatokea kuwa

Maneno haya yalitumika hapa kuonesha mwanzo wa simulizi mpya.

katika mwaka wa saba

Huu ni mwezi wa saba kwa Kalenda ya Kiebrania. ni mwishoni mwa mwezi wa Septemba na mwanzoni mwa mwezi octoba.

Ishmaeli ... Nethania ... Elishama ... Gedalia ... Ahikamu

Haya ni majina ya watu.

Jeremiah 41:4

Watu themanini "

"watu 80"

mikononi mwao

"mikono" inawakilisha watu. "katika umiliki wao"

Jeremiah 41:6

alipokuwa akiwakaribia

"Ishmaeli alipokuwa akiwakaribia watu 80"

Ikatokea kuwa

Maneno haya yametumika kuonesha umuhimu wa tukio katika simulizi.

Ishmaili mwana wa Nethania akawachinja na kuwatupa katika shimo, yeye pamoja na watu aliokuwa nao

"Ishmaeli mwana wa Nethania na watu aliokuwa nao, waliwaua watu 80 na kuwatupa katika shimo"

Jeremiah 41:8

watu kumi kati yao

Hawa ni kati ya wale watu 80

mahitaji

Ni vitu ambavyo vinatumika kwa mahitaji ya baadae.

Jeremiah 41:10

Ishmaeli ... Nebuzaradani ... Gedalia ... Ahikamu ... Nethania

Haya ni majina ya watu.

Jeremiah 41:11

Yohana ... Karea

Haya ni majina ya watu.

Wakampata

"wakampata Ishmaeli na watu wake"

Jeremiah 41:13

Kisha ikatokea kuwa

Maneno haya yalitumika kuonesha umuhimu wa tukio katika simulizi.

Ishmaeli ... Yohana ... Karea

Haya ni majina ya watu.

Jeremiah 41:15

Ishmaeli ... Nethania ... Gedalia ... Ahikamu

Haya ni majina ya watu.

Yohana ... Karea

Haya ni majina ya watu.

Wao waliokombolewa toka kwa Ishmaeli

"yeye na jeshi lake walikombolewa toka kwa Ishmaeli"

Hii ni baada ya Ishmaeli kumuua Gedalia mwana wa Ahikamu.

Mwandishi anaacha kusimulia na kuonesha tukio lililopita ili mtiririko wa matukio ueleweke.

Jeremiah 41:17

Geruthu ... Kimhamu

Hili ni jina la mahali.

Kwa sababu ya Wakaldayo

"kwa sababu walifikiri kuwa wakalfayo watawavamia"

msimamizi wa ardhi

"msimamizi wa ardhi ya Yuda"

Jeremiah 42

Jeremiah 42:1

Taarifa ya jumla:

Tazama: uandishi wa shairi.

Yohana ... Karea ... Yezania ... Hoshia

Haya ni majina ya watu.

watu wote toka kuanzia wadogo mpaka wakubwa

Hii inaonesha kuwa ni watu toka katika madaraja yote.

Maombi yetu yakubaliwe mbele yako

"tuyawakilishe maombi yetu mbele yako"

Jeremiah 42:4

Tazama

"kuwa makini kwa kile ntakachokizungumza"

Sitabakiza chochote

"nitakwambia kilakitu ambacho Bwana ameniambia"

Kweli na aminifu

Maneno haya yana maana inayofanana katika muktadha huu. Yanamuelezea Bwana kama shahidi ambaye hakuna atakayeweza kumuingilia. "anayeaminika"

Ikiwa ni nzuri au mbaya

Watu wanasisitiza kuwa watatii jibu litakalotoka kwa Bwana. "jibu lolote"

Sauti ya Bwana Mungu wetu

Bwana anaelezewa kwa namna anavyowajibu maswali yao.

Jeremiah 42:7

Neno la Bwana lilikuja

"Bwana anazungumza neno lake"

Watu wote kuanzia wadogo mpaka wakubwa

Hii inaonesha kuwa ni watu toka katika madaraja yote.

Nitapeleka maombi yenu mbele yake

"Nitawasilisha maombi yenu mbele yake"

Nitawajenga na sio kuwabomoa

Bwana anawafananisha wana wa Israeli kama ukuta unaoweza kujengwa au kubomolewa. "niwawastawisha na sio kuwaangamiza"

Nitawapanda na sio kuwang'oa

Bwana anatumia mfano huu kuonesha kuwa atawastawisha wana wa Israeli na sio kuwaharibu"

Nitaondoa maafa niliyoyaleta kwenu

Hapa Maafa yamezungumziwa kama kitu ambacho mtu anaweza kuweka juu ya mtu mwingine.

Jeremiah 42:11

Kuwaokoa na kuwakomboa

"kuokoa" na "kuwakomboa" yana maana sawa kusisitiza kuwa Bwana atawakomboa.

Kuwakomboa toka kwenye mkono wao

Hapa "mkono" inamaanisha nguvu na mamlaka.

Jeremiah 42:13

Ikiwa hamtaisikia sauti yangu, sauti ya Bwana Mungu wenu

Kutokutii ni sawa na kutosikia amri za Bwana.

ambapo hatutaona vita tena, ambapo hatutasikia sauti ya tarumbeta

Sentensi hizi zinaonesha kuwa vitani kwa uwezo wa kuona na kusikia.

hatutapata njaa

Kupata njaa ya chakula inaelezea uhaba wa chakula.

Jeremiah 42:15

upanga mnaouogopa utawapata

"mtaona matokeo mabaya sana ya vita huko"

Njaa mliyokuwa mkiiogopa itawafuata Misri

"Mlikuwa na hofu juu ya njaa Israeli lakini mkienda Misri mtateseka kwa njaa huko"

watu wote

Hawa ni watu wote kwa kuwa ni viongozi katika familia zao"

Jeremiah 42:18

Ghadhabu na hasira yangu imemwagwa

"Nimeimwaga ghadhabu na hasira yangu"

ghadhabu yangu na hasira yangu

"ghadhabu" na "hasira" vina maana moja.

hasira yangu itamwagwa juu yenu

"nitaimwaga hasira yangu juu yenu"

chombo cha kulaani na hofu, chombo cha kusema laana na mambo ya aibu

Maneo haya yana maana inayofanana yakisisitiza namna ambavyo mataifa mengine watawafanyia watu wa Yuda baada ya Bwana kuwaadhibu.

Nimekuwa shahidi

Bwana ndiye anayehakikisha kuwa wana wa Israeli wanaadhibiwa ikiwa hawatatimiza ahadi tao ya kutii amri za Bwana.

Jeremiah 42:20

tutachukua

"tutafanya"

mmtakufa kwa upanga

Vita imeelezewa kwa kutumia silaha inayotumika katika mapigano. "Mtakufa vitani"

sehemu ambayo mlitamani kwenda kuishi

"Misri ambapo mlifikiri kuwa mtakuwa salama"

Jeremiah 43

Jeremiah 43:1

Taarifa ya jumla:

Tazama: uandishi wa shairi.

Ikatokea kuwa

Hii ilitumika kuonesha mwanzo wa simulizi mpya.

Hoshaya ... Yohana ... Karea ... Neria

Haya ni majina ya watu.

kuchochea

"kumsababisha mtu awadhuru watu wengine"

Jeremiah 43:4

kukataa kusikiliza sauti ya Bwana

"hawakutii amri za Bwana"

ambapo walikuwa wametawanyika

"ambapo Bwana alisababisha wakaenda na kutawanyika"

Nebuzaradani ... Gedalia ... Ahikamu ... Shafani

Haya ni majina ya watu.

Tahpanesi

Hili ni jina la mji.

Jeremiah 43:8

Neno la Bwana lilikuja

"Bwana anazungumza neno lake"

Nitaweka ufalme huu juu ya mawe haya ... hema yake juu yao

"ufalme" na "hema" vilitumika kuonesha mamlaka ya kifalme.

hema

hema kubwa

Jeremiah 43:11

Taarifa ya jumla:

Bwana anaendelea kusema ujumbe wake.

atakuja

"Nebukadreza atakuja"

walioandikiwa kufa watakufa

"watakufa wote ambao nimeamua wafe"

walioandikiwa kwenda mateka watakwenda mateka

"Babeli watawachukua mateka wale wote nitakaoamua waende mateka"

Na aliyeandikiwa upanga atakufa kwa upanga

"Watakufa wote vitani ambao nimeamua wafe vitani"

Atasafisha nchi ya Misri kama ambavyo wachungaji wanavyosafisha nguo zao

"Atachukua kila kitu cha thamani toka Misri kama ambavyo mchungaji anavyotoa kwa makini wadudu kwenye nguo yake"

Heliopolisi

Hili ni jina la mji, "mji wa jua"

Jeremiah 44

Jeremiah 44:1

Taarifa ya jumla:

Tazama: uandishi wa shairi.

Hili ndilo neno lililomjia Yeremia

"Huu ndio ujumbe ambao Bwana alimpa Yeremia"

Mogdoli ... Tahpanesi ... Nofu ... Pathrosi

Haya ni majina ya miji.

Ninyi wenyewe mmeona

Neni "wenyewe" limetumika kusisitiza kuwa ni watu wa Yuda wanaoishi katika nchi ya Misri.

Tazama

"Sikiliza" au "kuwa makini" au "hakikisha unalielewa hili."

walitenda ili kuniudhi

"watu wa Yerusalemu na miji yote ya Yuda walitenda ili kuniudhi"

wao wenyewe

"watu wa miji iliyoharibiwa"

Jeremiah 44:4

Hivyo nikawatuma tena

Huyu ni Bwana.

hasiya yangu na ghadhabu yangu ilimwagika

Hii inaelezea hukumu ya Bwana kama maji ambayo ameyahifadhi kwenye maji lakini hasira yake inaweza kusababisha akaimwaga hasira yake kwa kuanza kuwahukumu wale wanaomkasirisha.

hasira yangu na ghadhabu yangu

"hasira" na "ghadhabu"yana maana moja yakiwa yanasisitiza uzito wa hasira yake.

Wakawa magofu na ukiwa

Maneno "magofu" na "ukiwa" yana maana sawa. yanasisitiza namna ambavyo Yuda na Yerusalemu itakuwa ukiwa.

Jeremiah 44:7

Kwa nini unafanya uovu mkuu juu yao? Kwa nini mnajikatilia wenyewe kati ya Yuda - wanaume, wanawake na watoto?

Bwana anatumia maswali haya kuwaambia wana wa Israeli kuwa wanapaswa kuacha kufanya mambo yatakayosababisha wahukumiwe.

matendo ya mikono yenu

"kwa mliyoyafanya"

mtaangamizwa

"mnasababisha niwaangamize"

Jeremiah 44:9

Mmesahau maovu yaliyofanywa na baba zenu na uovu uliofanywa na wafalme wa Yuda na wake zao?

"mmesahau uovu ambao baba zenu waliufanya! mmesahau uovu ambao wafalme wa Yuda na wake zao waliufanya."

Mmesahau uovu mlioufanya na wake zenu ... Yerusalemu?

"mmesahau uovu ambao ninyi na wake zenu mmeufanya ... Yerusalemu."

Mitaa ya Yerusalemu

Yerusalemu imezungumzwa kama sehemu ya mji ambapo watu hutembea.

Jeremiah 44:11

nitaelekeza uso wangu dhidi yenu

"kuamua kuwa kinyume nao"

wataanguka

Hii ni namna nyingine ya kusema kuwa watakufa.

Kwa upanga

Vita inaelezwa kwa kutumia silaha inayotumiwa mara nyingi na askari.

Toka mdogo mpaka mkubwa

Watu wote wasiokuwa na maana na wenye heshima katika jamii.

Jeremiah 44:13

upanga, njaa na tauni

Neno "upanga" linaelezea vita.

wakimbizi au waliopona

Haya maneno yote yanafanana. Mkimbizi ni mtu anayemtoroka mtu anayetaka kumuua au kumchukua mateka.

Jeremiah 44:15

Pathrosi

Hili ni jina la dini katika Misri.

Kuhusu neno ulilotuambia kwa jina la Bwana: Hatutakusikiliza

"Hatutatii amri ambayo ulitupa kwa mamlaka ya Bwana"

Malkia wa mbingu

Hiki ni cheo alichopewa mungu aliyeabudiwa Misri ambapo mungu huyo ni mwezi.

Kisha tutakuwa na chakula na kufanikiwa, bila kupata maafa yoyote

"katika siku hizo tulikua na chakula cha kutosha na mafanikio na hatutapata maafa"

Tutakuwa na chakula cha kutosha

"tutashibishwa vyema"

Kisha tutakuwa na chakula na kufanikiwa, bila kupata maafa yoyote

Watu wa Yuda walifikiri kuwa watafanikiwa kwa sababu malkia wa mbingu atawabariki ikiwa watamuabudu.

Jeremiah 44:18

Taarifa ya jumla:

Watu waliosalia waliokuwa wakiishi Misri wanaendelea kuongea.

Malkia wa mbingu

Hiki ni cheo alichopewa mungu aliyeabudiwa Misri ambapo mungu huyo ni mwezi.

je tunafanya mambo haya bila waume zetu kufahamu?

Wanawake wanajitetea kwa sababu wamepata ruhusa toka kwa waume zao.

Jeremiah 44:20

Bwana alikumbuka

"Bwana alikumbuka"

moyoni mwake

Hii ina maana kuwa Bwana alilikumbuka hili.

Jeremiah 44:22

Hwakuweza kuvumilia

"hawakuweza kuvumilia tena"

hakuna mwenyeji tena hata leo

"hakuna anayeishi huko sasa"

kufukiza uvumba

"kuteketeza sadaka kwa miungu ya uongo"

Hamtaisikia sauti yake

"sauti" ni amri za Bwana. "hamtatii amri zake"

Jeremiah 44:24

sema kwa kimywa chakeo na yabebe kwa mikono yako hayo uliyoyasema

"sema na utende kama ulivyosema"

Malkia wa mbingu

Hiki ni cheo alichopewa mungu aliyeabudiwa Misri ambapo mungu huyo ni mwezi.

Jeremiah 44:26

Tazama, niapa kwa jina kuu- asema Bwana

Jina kuu la Bwana linaonesha ukuu wake.

Kila mtu wa Yuda ... ataangamizwa

"Idadi kubwa ya watu wa Yuda ... wataangamizwa"

kwa uoanga na njaa

"upanga" inawakilisha watu watakaokufa vitani na "njaa" inawakilisha watu watakaokufa kwa njaa.

Jeremiah 44:29

Maneno yangu yatakuvamia kwa maafa

"ninayosema yatakupana na utapata maafa"

Nitamtia mfalme Farao Hofra mfalme wa Misri katika mikono ya adui zake

"nitawaruhusu maadui wa Farao Hofra wakukamate"

Hofra

Hili ni jina la mtu.

na wanaoyatafuta maisha yake

"na watu wanaotaka kumuua"

Jeremiah 45

Jeremiah 45:1

Taarifa ya jumla:

Tazama: uandishi wa shairi.

Baruki ... Neria

Haya ni majina ya watu.

aliyoambiwa na Yeremia

Baruku aliandika maneno ambayo Yeremia alisema.

Katika mwaka wa nne wa Yehoakimu

"wakati ambao Yehoakimu aliitawala Yuda kwa miaka minne"

alisema

"Yeremia alimwambia Baruku"

umeongeza uchungu katika maumivu yangu

"umenisababishia maumivu makubwa"

Nimechoka kuugua

"nimechoka kulia"

Jeremiah 45:4

Hivi ndivyo utakavyomwambia

Bwana anamwambia Yeremia jambo atakalomwambia Baruku.

Hii ni kweli juu ya dunia yote

"hili litatokea juu ya dunia yote"

Lakini je mmetegemea mambo makuu kwa ajili yenu wenyewe?

"mmetegemea kufanya mambo makuu kwa ajili yenu wenyewe"

Tazama

"kuwa makini"

nyara

Vitu vilivyoibiwa mahali kwa nguvu

maisha yako kama nyara

"Nitawaruhusu muishi. Hivyo ndivyo mtakavyotegemea.

Jeremiah 46

Jeremiah 46:1

Kwa ajili ya Misri

Hii inaonesha kuwa ujumbe ni kwa ajili ya taifa la Misri.

Karkemishi

Karkemishi ni mji ulioko mashariki mwa mto Efrate.

Lijamu

Hii inamaana ya kumuandaa farasi kwa ajili ya kuvuta gari.

Chepeo

Hii ni kofia ya kivita inayolinda kichwa katika vita.

Inoeni mikuki

Hii inamaana ya kuwa kuifanyia mikuku kuwa mikali.

Jeremiah 46:5

Taarifa ya jumla:

Maono ya Yeremia juu ya Misri yanaendelea.

Nini ninachokiona hapa?

Bwana anatumia swali kusisitiza kuwa anayoyasema juu ya Misri ni kweli.

wepesi hawawezi kukimbia na askari hawawezi kutoroka

Sentensi hizi mbili zina maana sawa zikisistiza kuwa hakuna anayeweza kukimbia awe mwenye nguvu au mwepesi.

Jeremiah 46:7

Taarifa ya jumla:

Yeremia anaendelea kunukuu maneno ya Bwana kwa taifa la Misri.

Huyu ni nani anayeinuka kama mto Nile

"Misri anainuka kama mto Nile." Bwana anauliza hili swali ili kuwafanya wasikilizaji wawe makini na taifa la Misri.

Misri imeinuka kama mto Nile

Jeshi la Misri linasababishwa na uharibifu unaosababishwa na mafuriko ya mto Nile.

Unasema

Hapa nchi ya Misri inazungumza kama mtu azungumzapo.

"Nitakwenda juu; nitaifunika nchi. Nitaharibu mji na wakaao ndani yake."

Hapa taifa la Misri linajisifu na kusema kuwa jeshi lake litaharibu dunia kama mafuriko.

kwenda juu, farasi. kukasirika, magari yenu.

Bwana anaamuri farasi na magari kama vile anaamuru watu. maneno haya "farasi" na "magari" yamezungumziwa kama sehemu ya vita.

Kushi ... Puti ... Ludimu

Haya ni majina ya biblia ya nchi za Ethiopia, Libya na Lydia.

kukunja pinde zao

Hiki ni kitendo cha kuupindisha upinde wenye mshale.

Jeremiah 46:10

Taarifa ya jumla:

Yeremia anaendelea kunukuu maneno ya Bwana kwa taifa la Misri.

Siku hiyo

Hii ni siku ambayo Wamisri watashindwa vita na Babeli.

maadui

Neno hili lina maanisha maadui wa Bwana.

upanga utateketeza na kuridhika. utakunywa damu yao

Hapa upanga unakula kama ambavyo mtu hula. sentensi hizi zinasisitiza kuwa kutakuwa na uharibifu kabisa.

upanga utateketeza

Neno "upanga" linawakilisha jeshi la taifa la Babeli.

Sadaka kwa Bwana

"Misri itakuwa sadaka kwa Bwana Mungu."

Jeremiah 46:11

Taarifa ya jumla:

Bwana anamaliza kusema ujumbe wake kwa Misri.

mabikira wa Misri

"wasioharibika wa Misri."

Kulaumiwa

Hii ni hali ya kujisikia aibu au kupoteza heshima yako.

Dunia imejawa na maombolezo yako

Kila mtu anasikia kilio chako.

Jeremiah 46:13

Migdoli ... Nofu ... Tahpanesi

Hii ni miji muhimu ya kivita. Nofu ulikuwa mji mkuu wa Misri.

Upanga umeteketeza wote

"jeshi la Babeli limesababisha uharibifu."

Jeremiah 46:15

kwa nini mungu wenu Api amekimbia?

"mungu wenu Api amekimbia."

Api

Huyu ni mmoja wa wakuu wamiungu ya Misri.

Kwa nini mungu wenu- ndama hasimami?

"mungu wenu ambaye ni ndama hawezi kusimama."

Bwana amemtupa chini

"Bwana amemshinda Api, mungu wenu wa ndama."

upanga huu umetupiga chini

"upanga" unawakilisha taifa la Babeli.

Farao mfalme wa Misri ni kelele tuu, ambeye aliacha nafasi ipite

Sentensi hii inasema kuwa taifa la Misri limepoteza umuhimu.

Jeremiah 46:18

mtu atakuja ambaye atakuwa kama mlima tabori na mlima Karmeli karibu na Bahari

Hili ni taifa la Babeli ambalo litaisonga taifa la Misri kama milima hii miwili.

Kusanya vitu vyako

"jiandae kusafiri.

Jeremiah 46:20

Misri ni ndama mzuri

Misri inafananishwa na ndama mzuri.

wadudu wakali

Hili ni jeshi la Babeli. Wadudu wakali watasababisha maumivu lakini sio maumivu ya kudumu.

askari ni kama ng'ombe aliyenona

Mwandishi anawafananisha askari kama "mg'ombe aliyenona" kwa sababu askari wanatunzwa vizuri.

Hawatasimama pamoja

Mwandishi anasema kuwa askari hawatapigana wakiwa na umoja lakini watakimbia wakifikiria kujiokoa wenyewe.

Misri wana sauti kama nyoka na hutambaa mbali

Mwandishi anasema kuwa taifa la Misri ni kama nyoka ambae hawezi kufanya chochote zaidi ya kutoa sauti na kutambaa kwa hofu wakata misitu wanapoingilia kiota chao.

Jeremiah 46:23

Watakata misitu

Jeshi la uvamizi litakuwa kama wakata mbao likikata msitu wote. "Jeshi la Babeli litaiangamiza miji ya Misri."

wao

Hili ni jeshi la taifa la Babeli likivamia Misri.

Hivi ndivyo alivyosema Bwana

"Alichokisema Bwana"

Ni nzito sana

Hii inaelezea idadi kubwa ya miji ya Misri.

Nzige

Hii ni aina ya wadudu wanaosafiri katika kundi kubwa na kusababisha uharibifu kwa kula mazao.

mabinti ... watapata aibu

Yeremia anasema kuwa watu wa Misri watapata aibu mbele ya mataifa hasa wanawake na mabinti watatendewa vibaya na askari wa Babeli.

mkono wa watu toka kaskazini

"nguvu ya taifa la Babeli lililotoka Kaskazini."

Jeremiah 46:25

Amoni wa Tabesi

Amoni ni mfalme wa miungu ya Misri. Tabesi ni mji mkuu wa Misri na hapa inawakilisha himaya yote ya Misri.

Ninawaweka ... kwenye mkono ya Nebukadreza na watumishi wake

Hapa Nebukadreza anawakilisha taifa zima la Babeli na "mkono" inawakilisha "kutawala"

Baada ya hayo Misri itakaliwa kama zamani

"Baada ya adhabu ya Bwana taifa la Misri litarudi na kuwa huru."

Hivi ndivyo alivyosema Bwana.

"Alichokisema Bwana"

Jeremiah 46:27

Mtumishi wangu Yakobo usiogope. Usifadhaike, Israeli

Sentensi hizi mbili zina maana moja. Pamoja zinawapa nguvu watu wa Yuda kuwa wasiogope.

Hivi ndivyo alivyosema Bwana

"Alichokisema Bwana"

Hatawaacha bila kuwaadhibu

"atawaadhibu ninyi"

Jeremiah 47

Jeremiah 47:1

Tazama

Neno "tazama" linatuonesha kuwa tunapaswa kuwa makini kusikiliza ambacho kinazungumzwa.

Mafuriki ya maji yanainuka toka kaskazini. Yatakuwa kama mto uliyojaa!

Sentensi hizi zinamaana moja. "maji" na "mto" vinawakilisha jeshi linalokuja toka kaskazini.

vitaijaza nchi

Hili ni jeshi linalotoka kaskazini.

Jeremiah 47:3

Kwa sauti za kukanyaga za farasi wao, kwa mwendo wa magari yao na sauti za magurudumu yao

Kwa pamoja vinawakilisha sauti za jeshi linalokuja.

mwendo wa magari yao na sauti za magurudumu yao

Maneno haya yametumika ili kuonesha msisitizo.

Kaftori

Hili ni jina la kisiwa kilichopo kaskazini mwa Wafilisti.

Jeremiah 47:5

upaa

Hiki ni kitendo cha kunyoa nywele zote za kichwani au sehemu ya nywele kama ishara ya maombolezo makubwa yanayofanywa na wanaoabudu sanamu wa mataifa kama Filisti.

watu ... watanyamaziswa.

"Watu ... watauawa."

Kwa muda gani mtajikata wenyewe kwa ajili ya kuomboleza

Kujikata ngozi ilikuwa inafanywa na wanaoabudu sanamu walipokuwa wakiomboleza msibani.

upanga wa Bwana

Hili ni jeshi ka kaskazini ambalo Bwana analitumia kuwaadhibu Wafilisti.

Itachukua muda gani mpaka mtakapokuwa kimya

Wafilisti walitumia swali hili kuonesha namna ambavyo walichanganyikiwa kutokana na uharibifu uliosababishwa na adui zao.

wewe

Hapa upanga wa Bwana unafananishwa na mtu.

ala

Ni kifaa kinachotumika kulindia makali ya upanga.

Ukuwaje kimya, kwa kuwa bwana amekuamuru

Hapa unazungumziwa upanga wa Bwana.

Jeremiah 48

Jeremiah 48:1

Mebo

Hili ni jina ;a moja ya Mlima huko Moabu.

Kiriathaimu

Hili ni jina la mji katika Moabu.

Kiriathaimu imekamatwa na kuaibishwa.

"Adui ameukamata mji wa Kiriathiamu na watu wake hawajivunii tena."

Heshima ya Moabu haipo tena

Hii ina maana kuwa heshima ya Moabu ambayo alikuwa akiifurahia imetoweka.

Heshboni

Hili ni jina la mji wa mfalme wa Waamori.

Madmena pia ataangamia

"madmena" ni mji uliopo Moabu. "Adui zao wataharibu mji wa Madmema."

Upanga utakufuata

Hii inmaanisha kuwa jeshi litaivamia Moabu.

Jeremiah 48:3

Taarifa ya jumla:

Yeremia anaendelea kuzungumza juu ya uharibifu wa Moabu.

Horonaimu

Hili ni jina la mji uliopo kusini mwa Moabu.

uharibifu na maangamizo makubwa

Maneno haya yana maana inayofanana. Yanasisitiza uharibifu.

Watoto wake

Hawa ni watu wa Moabu.

Luhithi

Hili ni jina la mahali huko Moabu.

Kwa sababu ya uharibifu

"kwa sababu ya uharibifu wa mji."

Jeremiah 48:6

Okoeni maisha yenu

Hapa wanazungumziwa watu wa Moabu.

mkawe kama mtu aliye mkiwa

Watu waliokimbia uharibifu katika mji wanafananishwa na kichaka kilichostahimili nyakati ngumu jangwani na chenye majani ya kijani mwaka mzima.

amini matendo yako

"kuishi kwa kufuata tamaduni na mafundisho ya dini yako"

Kemoshi

"Kemoshi" ni mungu mkuu wa Wamoabu. Hapa Kemoni inawakilisha taifa la Moabu.

Jeremiah 48:8

Basi bonde litaangamia na sehemu ya wazi itaharibiwa

Sentensi hizi zinafanana zikiwa zinasisitiza kuwa kila sehemu ya nchi itaharibiwa.

Mpe Moabu mbawa

"Wasaidie watu wa Moabu wakimbie."

kumwaga damu

"kuua watu"

Jeremiah 48:11

Moabu alijiona kuwa yuko salama tangu akiwa kijana

Hapa linazungumziwa taifa lote lla Moabu.

Yupo kama divai yake ambayo haijawekwa toka kwenye chombo kimoja hadi kingine

Hapa linazungumziwa taifa la Moabu ambalo linafananishwa na divai ambayo haikuhamishwa toka kwenye nchi yake.

Kwa hivyo analadha nzuri kuliko kawaida; ladha yake haibadiliki

Maneno haya yana maana moja.

Tazama, siku zinakuja

"Sikiliza kwa makini kwa sababu siku sio nyingi"

Hivi ndivyo alivyosema Bwana

"alichokisema Bwana"

watapiga juu yake na kumimina yote yaliyopo kwenye vyombo vyake na kuvunja mitungi yake

Maneni haya yanaonesha uharibifu unaokuja katika nchi ya Moabu.

Jeremiah 48:13

Mtasemaje

Hapa wanazungumziwa askari wa Moabu

Mtasemaje, 'sisi ni askari, wapiganaji wenye nguvu'"

"Hamuwezi kuendelea kusema, 'sisi ni askari wapiganaji wenye nguvu.'"

Jeremiah 48:15

vijana wake wazuri wamekwenda chini sehemu ya kuchinjwa.

"Vijana wao wazuri watachinjwa wote."

Uharibifu wa Moabu umekaribia kutokea; msiba unakuja haraka

"Maadui wa Moabu watawaangamiza haraka"

fimbo yenye nguvu, fimbo ya heshima, imevunjika

"Fimbo" imeelezewa kama nguvu na msaada wa kisiasa ambao Moabu aliutoa kwa mataifa mengine.

Jeremiah 48:18

Kaa katika nchi kavu, ewe binti unayeishi Diboni

Neno "binti" limetumika kuwaelezea watu wa Diboni.

ambaye ataharibu Moabu

"adui wa watu wa Moabu"

Waulize ambao

"waulize watu" au "waulize wanawake na wanaume"

Lia na kuomboleza

"lia kwa nguvu kwa maumivu na hasira"

Jeremiah 48:21

Holoni, Yasa, na ,Mefaasi ... Bozra

Hii ni miji ya Moabu.

Pembe ya Moabu imefungwa; jeshi lake limevunjwa

'pembe' na 'jeshi' vina maana moja. Inamaanisha kuwa Moabu amejeruhiwa.

Anachosema Bwana

Anachosema Bwana

Jeremiah 48:26

Kumfanya alewe

Adhabu ambayo Mungu ameituma kwa Moabu itawafanya wadharauliwe na adui zao, kama vile mlevi adharauliwavyo na kuchekwa.

Sasa Moabu atayaonea kinyaa matapishi yake, hivyo amekuwa kicheko

Mungu anaendelea kumfananisha Moabu na mlevi.

Je Israeli hajawa kicheko?

"Kwa kuwa mlikuwa mkiwacheka na kuwadharau watu wangu wa ufalme wa Israeli."

Je alikuwepo kati ya wezi, ambae ulikuwa unatikisa kichwa chako ulipokuwa ukizungumza kuhusu yeye?

"Japokuwa walikuwa wezi hawakukamatwa. Ulitikisa kichwa na kuwadharau.

Jeremiah 48:28

Maporomoko

Maporomoko ni sehemu yenye mteremko mkali katika mlima.

Kinywa cha shimo katika miamba

Huu ni uwazi uliopo katika miamba kama sehemu ya kuingilia katika pango.

Kiburi ... jeuri ... majivuno ... utukufu ... kujifurahisha moyoni mwake

Maneno haya yana maana inayofanana kwa pamoja yanasisitiza kiburi cha watu wa Moabu.

Jeremiah 48:30

Anachokisema Bwana

"alichokisema Bwana"

ukaidi

Ni kitendo cha kukataa kumtii mtu au maelekezo kwa sababu ya kiburi

Nitamlilia Moabu, na nitapiga kelele za huzuni kwa ajili ya Moabu wote

Yeremia anasema kitu kile kile kwa ajili ya kusisitiza.

Piga kelele

Kilio na huzuni ambacho mtu hufanya anapokuwa na uchungu.

Kir-heresi

Hili ni jina la mji wa zamani wa Moabu.

Jazeri ... Sibma

Haya ni majina ya miji miwili ya Moabu.

Jeremiah 48:33

sherehe na furaha vimeondolewa

"hakuna atakayekuwa na raha wala kufurahia huko Moabu"

Nimeufanya kuwa mwisho

"Nimesimamisha"

Hawatatembea

"hawatakanyaga" Hawa ni watengeneza mvinyo wa Moabu.

Jeremiah 48:34

Heshiboni

Hili ni jina la mji wa kifalme wa mfalme wa Moabu.

Eleale ... Yahasa ... Soari ... Horonaimu ... Eglath-Shelishia

Haya ni majina ya miji ya Moabu.

Nimrimu

Hili ni jina la mto karibu na bahari ya Shamu.

Analosema Bwana

"alilosema Bwana"

Jeremiah 48:36

Moyo wangu unaomboleza kwa ajili ya Moabu kama filimbi

Yeremia anafananisha hisia zake na wimbo wa huzuni.

Moyo wangu unaombileza

"moyo" inamaanisha hisia za ndani anazihisi Yeremia. "Nina huzuni sana kwa ajili yake."

Kir Heresi

Kir-Heresi ulikuwa mji wa zamani wa Moabu kama kilimeta 18 mashariki mwa bahari ya Shamu.

Kwa kila kichwa kuna kipara na ndevu zote zimenyolewa. Chale zipo katika kila mkono na magunia yanazunguka kiuno chake.

Haya ni mambo ambayo watu wa Moabu hufanya wanapoomboleza au kuwa na masikitiko.

Chale

Kukata ngozi

Jeremiah 48:38

Kila paa la gorofa

"kila paa"

uwanda

Ni sehemu ya wazi, kama vile sokoni.

kwa kuwa nimeiharibu

Bwana anazungumziwa mahali hapa.

Analosema Bwa

"Alilosema Bwana"

kuvunjwa

"kuharibiwa"

piga kelele

Sauti ya kilio ambayo huifanya mtu anapokuwa na maumivu.

Hivyo Moabu itakuwa kitu cha kudharauliwa

"Moabu itakuwa taifa ambalo mataifa ya jirani yatalicheka"

Jeremiah 48:40

Adui atapaa kama tai na kutandaza mabawa yake

Hii inalifananisha jeshi lenye nguvu litaivamia Moabu na kuiteka kama vile tai anaposhuka chini na kukamata mawindo.

Keriothi.

Ni mji katika Moabu.

Keriothi imekamatwa na ngome zake zimetekwa

"Adui wameikamata Keriothi na kuteka ngome zake"

siku ile moyo wa askari wa Moabu ... wanawake wenye uchungu

Sentensi hii inaonesha kuwa hofu itawapata askari wa Moabu kama hofu ambayo wanawake huipata wanapokaribia kuzaa.

Jeremiah 48:42

Hivyo Moabu itaharibiwa

"Hivyo adui atawaharibu watu wa Moabu"

katika mwaka wa

"Mwaka" inatafsiriwa kama "wakati" au "majira."

Analisema Bwana

"Alililosema Bwana"

Jeremiah 48:45

waliokwenda

Hawa ni watu walioweza kukimbia katika kipindi cha uharibifu wa Moabu.

Kivuli cha Heshiboni

sehemu salama katika mji wa Heshboni.

kwa kuwa moto utatoka Heshboni, miale toka katikati ya Sihoni

Hii ina maana kuwa uharibifu wa Moabu utaanza na kusambaa toka Heshiboni.

Paji la uso wa Moabu na juu ya vichwa vya watu wenye kujivuna

Hapa wanazungumziwa watu wa Heshboni na viongozi wao.

Paji la uso

Ni sehemu ya uso iliyoko juu ya macho. Ni ishara ya kujivuna.

Juu ya vichwa vya watu wenye majivuno.

Hapa wanazungumziwa watu muhimu wa Moabu kama wakuu na viongozi.

Jeremiah 48:46

Watu wa Kemoshi wameharibiwa

"Watu wa Kemoshi wameharibiwa na adui zao"

Kemoshi

"Kemoshi" ni mungu mkuu wa Wamoabu. Hapa Kemoni inawakilisha taifa la Moabu.

siku zijazo

Hizi ni siku za wakati ujao, zilizoitwa "siku za mwisho."

Analosema Bwana

"alilosema Bwana"

Jeremiah 49

Jeremiah 49:1

Taarifa ya jumla:

Tazama uandisi wa shairi.

Je Israeli hana watoto? Hakuna mrithi katika Israeli?Kwa nini Meloki ameitawala D=Gadi na watu wake waishio kwenye miji yake?

"Kuna Waisraeli wengi wa kurithi nchi ya Israeli. Watu waabuduo miungu ya uongo, Moleki hatakiwi kuishi Gadi."

Hivyo tazama

Hii inaongeza msisitizo wa jambo linalofuata. "Tazama na sikiliza"

Siku zinakuja

"Siku za baadae"

Anayosema Bwana

"Alilosema Bwana"

Jeremiah 49:3

Piga kelele

Lia kwa nguvu

Binti za Raba

Wanawake katika mji wa Raba

Kwa nini unajisifu kwa nguvu zako?

"Hutakiwi kujisifu kwa sababu hauna nguvu."

Nani atakuja dhidi yangu?

"Mnafikiri kuwa hakuna atakayewashinda."

Jeremiah 49:5

Wewe

Hawa ni watu wa Amoni.

tawanyika

"kwenda kwa uelekeo tofauti"

Analosema Bwana

"Alilosema Bwana"

Jeremiah 49:7

Ana ushauri mzuri ... uelewa? Je hekima yao iliharibiwa?

Wazo moja linaelezewa katika njia mbili tofauti.

Je ushauri mzuri umepotea kwa wale wenye uelewa?

"Inaonesha kuwa hakuna tena watu wenye hekima Temana katika Edomu!"

Je hekima yao iliharibiwa?

"Ushauri wao hauna hekima tena."

Jeremiah 49:9

Taarifa ya jumla:

Bwana anaendelea kuzungumza kuhusu kitakachotokea Edomu.

Kama wavunaji wa zabibu watafika

"Wale wanaovuna zabibu huwa wanaacha baadhi kwenye mizabibu."

Wezi wakija

"Wezi wakija usiku, wataiba kwa kadiri wanavyohitaji"

Jeremiah 49:12

Taarifa ya jumla:

Bwana anaendelea kuzungumza kuhusu kitakachotokea Edomu.

Tazama

"Kuwa makini"

Kunywa kikombe

"pata adhabu"

Je unafikiri kuwa utakwenda bila kuadhibiwa?

"Unapaswa kufahamu kuwa utapata adhabu yangu kwa sababu ya dhambi zako."

wewe ... mwenyewe

Hawa ni watu wa Edomu.

Analosema Bwana

"Alilosema Bwana"

Jeremiah 49:14

Taarifa ya jumla:

Sasa Yeremia anazungumza na watu wa Edomu.

Nimesikia

Hapa Yeremia anazungumza.

Kumvamia

Hapa anazungumziwa Edomu.

Nimefanya

Huyu ni Bwana.

Wewe

Hili ni taifa la Edomu.

Jeremiah 49:16

Taarifa ya jumla:

Bwana anaendelea kuzungumza kuhusu kitakachotokea Edomu.

Kiota cha juu kama tai

"Kuishi sehemu salama kama tai juu ya milima mirefu"

Analosema Bwana

"Alilosema Bwana"

Jeremiah 49:17

Taarifa ya jumla:

Bwana anaendelea kuzungumza kuhusu kitakachotokea Edomu.

Tetemeka

"Kutetemeka kutokana na kuogopa na kuzungumza mambo yao yasiyopendeza"

Kama kupinduliwa kwa Sodoma na Gomora

"Kwa njia ambayo Sodoma na Gomora waliharibiwa"

Hakuna atakayeishi huko; hakuna atakayekaa pale

Bwana anazungumza jambo lilelile mara mbili kusisitiza kuwa Edomu Edomu haitakuwa na watu kabisa.

Jeremiah 49:19

Taarifa ya jumla:

Bwana anaendelea kuzungumza kuhusu kitakachotokea Edomu.

Tazama

"Kuwa makini"

Kama simba

Hii ni namna nyingine ya kusema kuwa uvamizu utakuwa wa mkali na usiotarajiwa.

Je nani aliye kama mimi, na nani ataniita?

Bwana anatumia swali kuonesha udogo wa mwanadamu. "Hakuna aliye kama mimi, hakuna wa kuniamrisha."

kuita

"kumuamrisha mtu aje"

Ni mchungaji gani atakayeweza kuniamrisha mimi?

Bwana anatumia swali kuonesha kuwa hakuna wa kumshinda.

Jeremiah 49:20

Wenyeji wa Temana

Watu waishio Temana.

Watasukumwa nje hata kundi dogo

"Atawasukuma nje, hata kundi dogo"

Ardhi yenye malisho itakuwa sehemu iliyoharibiwa

"Atageuza sehemu zao wa malisho kuwa sehemu zilizoharibiwa"

Ardhi ya malisho

Hii ni sehemu yenye nyasi ambapo wanyama hula majani.

Jeremiah 49:21

Yao

Watu wa Edomu.

Kwenye sauti ya kuanguka kwaonchi ilitetemeka. Sauti ya dhiki ilisikika bahari ya Shamu

Hii inaonesha kuwa uharibifu wa Edomu utakuwa mbaya sana.

Tazama

"Kuwa makini"

kuvamia kama tai, kushambulia chini na kutandaza mbawa zake

Uvamizi utakuwa mbaya na usiotarajiwa.

Bozra

Huu ni mji.

Kuwa kama moyo wa mwanamke mwenye uchungu

"hisi kuharibiwa na hofu"

Jeremiah 49:23

Taarifa ya jumla:

Bwana anatuambia mambo yatakayotokea kwa watu wa Dameski.

Arpadi

Huu ni mji huko Sirya.

Waliyeyuka

"Walikuwa na hofu"

Wakawa wasumbufu kama bahari

Hisia zao zilifananishwa na bahari yenye mawimbi"

kama maumivu ya mwanamke anayejifungua

Namna mji unavyoteseka inafananishwa na mwanamke mwenye maumivu wakati wa kujifungua.

Kwa nini mji maarufu, mji ambao niliufurahia bado haujaondolewa?

"Haiwezekana mji maarufu, mji ambao ulikua na furaha bado una watu ndani yake."

Jeremiah 49:26

Taarifa ya jumla:

Bwana anatuambia mambo yatakayotokea kwa watu wa Dameski.

yake

"yake" inamaanisha Dameski.

Analosema Bwana wa majeshi.

"Alilosema Bwana"

Ben Hadadi

Hili ni jina la mfalme.

Jeremiah 49:28

Taarifa ya jumla:

Yeremia anazungumza juu ya mambo yatakayotokea kwa Kedari.

Kedari

Hili ni kundi la watu.

Hazori

Hii ni sehemu katika Biblia na ni Israeli ya sasa.

Jeremiah 49:30

Taarifa ya jumla:

Bwana anaendelea kuzungumza juu ya mambo yatakatotokea kwa Kedari.

Kaa katika mashimo ya ardhini

"jifiche"

Wenyeji wa Hazori

"Watu wanaoishi Hazori"

Analosema Bwana

"Alilosema Bwana"

Kupanga mpango

"kuweka mpango"

Wao ... wao

Hawa ni watu walioona usalama.

Jeremiah 49:32

kutawanyika kwenye kila upepo

"kwenda katika uelekeo tofauti"

Nitawatawanya kwenye kila upepo wale wote wanyoao denge

"Kisha nitawatawanya katika uelekeo tofauti wale wasiotoo amri zangu"

Hakuna atakayeishi huko, hakuna binadamu atakayekaa huko

Maneno haya yanasisitiza kuwa Hazoro itaharibiwa kabisa.

Jeremiah 49:34

Taarifa ya jumla"

Bwana anazungumza juu ya mambo yatakayotokea kwa Elamu.

watu wa upinde

Ni watu ambao wana ujuzi wa upinde na mishale.

pepo nne toka kwenye kona nne

"pepo 4 toka kwenye kona 4"

kona nne za

"Pando zote, kila mahali".

Hakuna taifa ambalo wale waliotawanyika toka Elamu hawatakwenda.

"Wakimbizi toka Elamu watalazimika kutafuta makazi kila sehemu duniani."

Jeremiah 49:37

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza juu ya mambo yatakayotokea kwa Elamu.

Analosema Bwana

"Alilosema Bwana"

tuma upanga

"tuma maadui ili wawaue"

Nitaweka ufalme wangu

"Nitaanzisha utawala wangu "

Jeremiah 50

Jeremiah 50:1

Taarifa ya jumla:

Tazama ushairi.

Kwa mkono wa Yeremia

"kwa matendo ya Yeremia"

wasababishe wasikie ... wasababishe wasikie

Kurudia huku kunasisitiza umuhimu wa amri hiyo.

Beli imeaibishwa, Merodaki imefadhaishwa. ,Mingu yao zimeaibishwa na sanamu zao zimefashaishwa

Sentensi hizi zinasisitiza kuwa Bwana ameiharibu miungu ya Babeli.

Beli ... Merodaki

Haya ni majina mawili ya miungu wakuu wa Babeli.

Jeremiah 50:3

Simama dhidi yao

Neno "yao" inamaanisha Babeli.

nchi yake

Neno "yake" inamaanisha Babeli.

Ishi ndani yake

Neno "yake" inamaanisha Babeli.

Siku hizo na wakati huo.

"siku hizi" au "wakati huo huo"

Watauliza

Hawa ni watu wa Israeli au Yuda.

tujiunge kwa Bwana

Hii lugha ya picha inayoonesha muunganiko wa kiroho kwa Bwana.

ambayo haitasahauliwa

"ambayo hakuna atakayeisahau"

Jeremiah 50:6

kundi la mwisho

Hii inawafananisha wana wa Israeli na kundi la kondoo waliopotea.

wakawameza wao

Hii inafananisha kuharibiwa na kuchukua kila kitu sawa na kitendo cha kula.

wamefanya dhambi

Hawa ni wana wa Israeli.

Jeremiah 50:8

Kama beberu anayeondoka

Hii inawafananisha wana wa Israeli ambao Bwana amewashauri waondoke mapema Babeli kama beberu anayeshangaa toka kwenye kundi.

Bebeli itakamatwa toka hapo

"Mataifa yataikamata Babeli"

Analosema Bwana

"Alilosema Bwana"

Jeremiah 50:11

Unaruka kama ndama anayekanyaga malisho yake

Hii inawafananisha watu wa Babeli kama ndama mwenye furaha.

Kukanyaga

sauti za jeshi linalokuja

Jirani yako kama farasi mwenye nguvu

Hii inafananisha furaha zao na furaha ambazo jirani zao wanapiga.

Hivyo mama yako ataaibika sana, aliyekuzaa anazalilika

Sentensi hizi zina maana moja zikisisitiza namna ambavyo aibu itakuwa kubwa.

jangwa, nchi kavu

Hii inasisitiza namna ambavyo nchi imekuwa tasa kabisa.

Tapatapa

Tetemeka kwa sababu ya hofu

Sonya

Kufanya sauti kama ya nyoka yenye maana ya kutokukubali.

Jeremiah 50:14

Taarifa ya jumla:

Bwana anawaambia maadui wa Babeli namna ya kuvamia.

Kila anayepindisha upinde

Hawa ni askari wanaopindisha upinde na mishale ili kupigana.

mpigeni

Hapa anazungumziwa Babeli.

Kuta zake zimeangushwa chini

"Mataifa yameangusha chini kuta zake"

Jeremiah 50:16

Taarifa ya jumla:

Bwana anawaambia maadui wa Babeli namna ya kuvamia.

yeye anayetumia mundu wakati wa mavuno.

"Mundu" ni kifaa kinachotumika wakati wa kuvuna nafaka. Bwana anasema kuwa kupanda na kuvuna hakutakuwepo Babeli.

Kila mtu arudi kwa watu wake ... warudi katika nchi yao

Maneno haya yanasisitiza kuwa wageni waende Babeli.

toka kwenye uoanga wa mtesi

Neno "upanga" linamaanisha adui ambao wataivamia Babeli.

Jeremiah 50:17

Israeli ni kondoo waliotawanyika na wamefukuzwa na simba

"Israeli ni kondoo ambao wametawanyishwa na simba"

mmeze

Hii inafananisha uharibifu wa Israeli kama kitendo cha kumeza.

alivunja mifupa yake

"Aliharibu Israeli"

Tazama, Ninataka

Neno "tazama" linamaanisha kuwa makini na kinachofuata.

Jeremiah 50:19

Nitarejesha

Bwana anazungumza.

atakula huko Karmeli na Bashani

"Israeli watakula chakula cha Karmeli na Bashani."

Siku hizo na wakati huo

"siku hizo" na "wakati huo huo"

uovu utaangaliwa katika Israeli lakini hautaonekana. Nitauliza juu ya dhambi za Yuda lakini hakuna atakayeziona

Sentensi hizi zina maana moja. Kwa pamoja zinasisitiza kuwa Bwana atasamehe kabisa maovu ya wana wa Israeli.

ovu utaangaliwa katika Israeli lakini hautaonekana.

"Bwana ataangalia uovu wa wana wa Israeli lakini hatauona"

Jeremiah 50:21

Merathaimu

Hili ni jina lingine la Babeli.

Pekodi

Hili ni jina lingine la Kaldayo.

Waweke kwenye upanga

"waue"

Analosema Bwana

"Alilosema Bwana"

Jeremiah 50:23

Kwa namna gani nyundo ya mikono yote imekatwa vipande na kuharibiwa

"nyundo wa mikono yote" ni jeshi kubwa la Babeli ambalo litakwenda kuharibiwa.

Hofu

Ni hisia nzito ya uoga na mshtuko.

Ulikamatwa, Babeli

"Nilikukamata, Babeli"

Ulionekana na kukamatwa

"Nilikuona na kukukamata"

Jeremiah 50:25

Ghala

Majengo ambayo nafaka zinahifadhiwa.

kusanya juu yake kama chungu cha nafaka

"kusanya juu yake kile kilichobaki kama zinavyokusanywa nafaka"

Jeremiah 50:27

Taarifa ya jumla:

Bwana anaendelea kuzungumza namna ya kuwaharibu watu wa Babeli na Kaldayo.

Ua ng'ombe zake wote

Askari vijana wanafanaishwa na ng'ombe kutokana na nguvu zao.

ng'ombe wao

"wao" inamaanisha Babeli.

wao ... yao

Hawa ni watu wa Babeli.

Wale

Hawa ni watu waliosalia toka Babeli ambao watawaambia wengine juu ya kisasi cha Bwana.

Jeremiah 50:29

Taarifa ya jumla:

Bwana anaendelea kuzungumza namna ya kuwaharibu watu wa Babeli na Kaldayo.

Yeye

Babeli anazungumziwa hapa.

Waoiganaji wake wataharibiwa

"Nitawaharibu wapiganaji wake"

Jeremiah 50:31

Tazama

Neno hili linatambulisha kitu hivyo umakini unahitajika.

Wanaojivuna

Bwana anawaelezea hivi watu wa Babeli.

Kwa kuwa siku yako imekuja ... muda ambao nitakuadhibu

Sentensi hizi zina maana inayofanana. "Kwa kuwa siku nitakayokuadhibu imefika"

Siku yako

Hii inaonesha muda ambao adhabu kubwa itakuja juu ya Babeli.

Nitaangaza

Bwana ataangaza

Moto katika miji yao

Hii inaonesha namna ambavyo uharibifu utatokea.

Jeremiah 50:33

Watu wa Israeli wamenyanyaswa

"Babeli wanawanyanyasa watu wa Israeli"

Kuwakamata

Hawa ni watu wa Israeli.

Walikataa

Hawa ni watu wa Babeli.

Kuwaacha waende

Hapa wanazungumziwa wana wa Israeli.

Jeremiah 50:35

Upanga uko juu ya Wakaldayo

"maadui wanakuja juu ya Wakaldayo"

Hili ndilo analosema Bwana

"Alilosema Bwana"

walijidhihirisha kama wapumbavu

Neno "kujidhihirisha" linaonesha kuwa matendo yao yalikuwa ya kipumbavu na watawekwa wazi ili kila mtu awaone.

watajawa na hofu

"hofu itawajaa"

watakuwa kama wanawake

"watakuwa dhaifu kama wanawake"

Chumba cha kuhifadhia

Chumba cha kuhifadhia ni sehemu ambayo vitu vya thamani vinawekwa.

Watachukuliwa nyara

"maadui watawateka nyara"

Jeremiah 50:38

maji yao

"maji" inawakilisha vyanzo vyote vya maji hasa mito inayopita kwenye mji.

Mbweha

Mbweha ni mbwa mwitu wanaopatikana Asia na Afrika.

Mbuni wataishi kwake

"mbuni" ni ndege mkubwa wa Afrika anayekimbia haraka lakini hawezi kupaa. Neno "kwake" linamaanisha Babeli.

Kwa muda wote hatakuwa mwenyeji. Kizazi hadi kizazi hakitaishi kwake.

Sentensi hizi zina maana inayofanana zikisisitiza kuwa Babeli haitakuwa na wenyeji kabisa.

Hataishi ndani yake

"hakuna atakayeishi kwake"

hakuna atakayeishi huko; hakuna atakayekaa kwake

Maneno haya yanamaana moja yakisisitiza kuwa Babeli haitakuwa na wenyeji kabisa.

Jeremiah 50:41

Tazama

Neno hili linaonesha kuwa makini kusikiliza anachosema Bwana.

taifa kubwa na wafalme wengi.

Hii inaonesha wakati ambao Medesi na Peru waliivamia Babeli katika mwaka wa 539 kabla ya Kristo.

kwa mpangilio kama watu wapambanaji

Namna ambavyo wapiganaji wanajipanga vitani.

Binti wa Babeli

Hawa ni watu wa Babeli.

Jeremiah 50:44

Tazama

Neno hili linaongeza msisitizo kwa jambo linalofuata.

Walikwenda juu

Hawa ni wavamiaji toka kaskazini.

Kama simba

Hii ni jina nyingine ya kusema kuwa uvamizi ulikuwa wa nguvu na usiotarajiwa.

Kwa haraka nitawafanya waikimbie

Hapa wanazungumziwa watu wa Babeli ambao watawakimbia wavamizi.

ambaye atachaguliwa

"ambaye nitamchagua"

Nani kama mimi, na nani atakayeniita?

Bwana anatumia swali kuonesha udogo wa mwanadamu. "Hakuna kama mimi, hakuna wa kuniamuru."

kuita

Kumuamuru mtu aje

Ni mchungaji gani atakayepambana na mimi?

Bwana anatumia swali kuonesha kuwa hakuna kiongozi wa kumpinga au kumshinda.

Jeremiah 50:45

Maamuzi ambayo Bwana ameamua kwa ajili ya Babeli , maamuzi ambayo Bwana ameamua kwa ajili ya nchi ya Kaldayo

Sentensi hizi zina maana inayofanana. "Maamuzi ambayo Bwana ameamua kwa ajili ya Babeli na Kaldayo.

Watatolewa nje

Hii inamaanisha kuwa watu wa Babeli watatolewa kwenye nyumba zao wawe wanataka au hawataki.

Nchi zao zenye malisho zitaharibiwa

"Nitazigaribu nchi zao za malisho"

Sauti ya kuivamia Babeli itatikisa dunia

Sentensi hii inafananisha anguko la taifa lenye nguvu sa

Jeremiah 51

Jeremiah 51:1

upepo wa uharibifu

"uhasibifu usio na mwisho"

Leb- Kamai

Hili ni jina lingine la Babeli.

Kutawanyika

Kutawanyika ni kusambaratisha na kwenda uelekeo tofauti.

Siku ya maafa

"siku itakapoharibiwa"

Jeremiah 51:3

Usiwaruhusu wapiga mishale kupindisha upinde wao

"Usiwaruhusu wapiga mishale kuandaa upinde"

Jeremiah 51:7

Babeli ilikuwa kikombe cha dhahabu

"Babeli lilikuwa taifa lenye nguvu lililotumika kwa ajili ya hukumu"

wazimu

"kutokuwa na uwezo wa kufikiri vizuri"

Kuomboleza

Hiki ni kilio cha nguvu chenye huzuni.

Jeremiah 51:9

Hatia yao imefika mbinguni, imefikia mawingu

"Babeli ina hatia sana"

Bwana ametamka haki yetu

Bwana aliiadhibu Israeli kwa sababu ya makosa yao lakini sasa amewaacha wamrudie.

Jeremiah 51:11

Wenyeji

Hawa ni watu wanaoishi sehemu fulani.

Jeremiah 51:13

Kuishi katika vijito vingi vya maji

"wanafuraha na utajiri"

Uzi ... mfupi

"maisha yako yatakwisha haraka."

kama pigo la nzige

"kwa idadi kubwa ya askari"

kilio cha vita

Hizi ni kelele ambazo askari huzifanya anapokuwa vitani.

Jeremiah 51:15

anapopiga radi, kuna sauti ya maji katika mbingu

Maneno haya yanaifananisha sauti ya Bwana na sauti kubwa ya radi na mvua.

Ghala

Ghala ni sehemu ambayo vitu hihifadhiwa kwa ajili ya matumizi ya baadae.

Jeremiah 51:17

Kila mtu alikuwa kama mnyama bila maarifa

Hii inaonesha hisia za Yeremia kuwa watu wanaoamini sanamu ni wapumbavu.

Udanganyifu

Uongo

Jeremiah 51:20

Wewe

"Jeshi la Babeli"

Jeremiah 51:22

Wewe

"Jeshi la Babeli"

Jeremiah 51:24

Kwnye machi yako

"Ninyi watu wa Babeli mtaona"

Analosema Bwana

"ambalo Bwana alilisema"

Jeremiah 51:25

Mlima

Bwana anazungumza na Babeli kama vile ulikuwa mlima anaoweza kuzungumza nao kama mtu. "taifa lenye nguvu"

Wengine

Hawa ni watu wote ambao wamevamiwa na Babeli.

Maporomoko

Maporomoko ni mteremko mkali wa mlima au kilima.

Jeremiah 51:27

Bendera

Hii ni bendera kubwa ambayo askari huifuata katika vita.

Yeye

"Babeli"

Mini ... Ashkenazi

Hata ni majina ya mataifa au watu katika makundi.

Leteni farasi kama nzige

"Leteni farasi wengi na askari haraka."

Jeremiah 51:29

Nchi itatetemeka

Bwana aliahidi mapinduzi makubwa ambapo nchi nzima itatetemeka.

Kuwa katika maumivu

Babeli itakuwa katika maafa makubwa.

Jeremiah 51:30

Huu mji umechukuliza

"Adui wameumiliki mji wote."

Vivuko katika mito yalitekwa

Adui walimiliki sehemu zote za kuvukia.

Vivuko

Kivuko ni sehemu nyembamba katika mto ambayo watu hutumia kupita.

Kuchanganyikiwa

"Kutokuwa na uwezo wa kufikiri vizuri"

Jeremiah 51:33

Binti wa Babeli

Ni jina lingine linalowakilisha Babeli.

Kama sakafu ya kufikichia

Bwana analinganisha kufikichia na wakati wa starehe wa Babeli.

Muda wa kuvuna utakuja kwake

Kuvuna ni matokeo ya matendo ambayo watu waliyafanya mwanzo. "Babeli itaadhibiwa."

Jeremiah 51:34

Amenikausha na kunifanya kuwa bakuli tupu

Babeli amechukua kila kitu cha Israeli.

Amenimeza

Yerusalemu inafananisha uharibifu wake na kitendo cha kumezwa.

Kama Joka

Hii inamfanaisha Babeli na Joka.

Anashibisha tumbo lake kwa chakula kizuri.

Hii inaelezea kuwa Babeli amechukua kila kitu toka kwa Israeli.

Amenitoa nje.

Ambacho Babeli hakukipenda baada ya kuchukua kila kitu ni kutupa vyakula vya zamani toka kwenye chugu.

Wenyeji wa Kaldayo

"watu walioishi Kaldayo."

Jeremiah 51:36

Taarifa ya jumla:

Hapa Bwana anaanza kujibu ombi la Yeremia katika mstari wa 34 na 35.

Miundo ya saruji

Haya ni majengo ambayo yamekuwa kama uchafu.

Kundi la mbweha

"nyumba kwa ajili ya mbwa mwitu"

maafa

"sehemu mbaya ya kuishi"

Sonya

Hii ni sauti inayoonesha kutokukubali.

Jeremiah 51:38

Nguruma

Hii ni sauti ya juu anayoitoa simba.

Ngurumo

Hii ni sauti ya kitisho inayotengenezwa na wanyama.

Analosema Bwana

"ambalo alilisema Bwana"

Jeremiah 51:41

Bahari ... mawimbi yavumayo

Maadui wa Babeli wamewakamata. "Mawimbi" yanawakilisha watu wengi wanaoivamia Babeli.

Jeremiah 51:43

Miji yao

"Miji ya Babeli"

Nitamuadhibu Beli

Beli alikuwa mungu wa Babeli na anawakilisha nchi nzima na watu wanaoiabudu.

toka kwenye kinywa chake alichokimeza

Bwana analinganisha sadaka na kafara zote a Beli na vitu alivyovila.

Mataifa hayatakwenda tena

Bwana anayafananisha mataifa mengi yanayokwenda bBabeli kutoa sadaka kwa beli kama mto unatotembea.

Jeremiah 51:45

Taarifa zilizosikika

Taarifa walizozisikia watu.

Kiongozi atampinga kiongozi.

Viongozi wanawakilisha taifa lililo chini ya utawala wao.

Jeremiah 51:47

Tazama

"kuwa makini"

Nchi yake yote

"Wato wote wa Babeli"

Mbingu na nchi

Mbingu na nchi vimetazamwa kama watu.

Analosema Bwana

"ambalo Bwana alilisema"

waliouawa

"watu waliouawa"

Jeremiah 51:50

Taarifa ya jumla

Yeremia anazungumza na watu wa Israeli katika sura ya 50.

matukano

"maneno ya kuumiza"

Jeremiah 51:52

Kilio

Kulia kwa sababu ya maumivu au huzuni.

Hata ... kwake

Hii ni njia ya kusema kuwa ni vigumu Babeli kuepuka hukumu ya Bwana.

Jeremiah 51:54

Sauti ya dhiki inatoka Babeli, anguko kuu toka kwenye nchi ya Wakaldayo

Wazo moja linaelezewa kwa njia mbili ili kuonesha msisitizo.

Sauti ya adui ni kama mawimbi ya maji mengi

Sauti ya maadui wanaokuja itakuwa kubwa sana.

mashujaa wake wamekamatwa

"Wamewakamata mashujaa wake."

Jeremiah 51:57

Yeye ... wao

Hawa ni watu wa Babeli.

Jeremiah 51:59

Seraya ... Neria ... Maaseya

Haya ni majina ya watu.

Jeremiah 51:61

Hakutakuwa na wenyeji, watu au wanyama

Wanyama wanaozungumziwa hapa ni wanyama ambao wanaishi na watu.

Jeremiah 51:63

Babeli itazama kama hivi

"Babeli itapotea kama jiwe hili linavyopotea."

Jeremiah 52

Jeremiah 52:1

Hemutali

Hili ni jina la mwanamke.

Libna

Hili ni jina la mji.

Yeremia

Huyu ni Yeremia mwingine na sio nabii Yeremia aliyeandika kitabu hiki.

Yeye

Huyu ni Sedekia anazungumzwa hapa.

Jeremiah 52:4

Ikawa

Hii imetumika hapa kuonesha mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

katika mwaka wa tisa

"katika mwaka wa tisa"

katika mwaka wa kumi, siku ya kumi ya mwezi

Huu ni mwaka wa kumi kwa kalenda ya Kiebrania. Siku ya kumi ni karibu na mwanzo wa Januari katika kalenda ya magharibi.

Waliweka kambi juu uakr

"jeshi la Nebukadreza liliweka kambi juu ya Yerusalemu"

Mpaka mwaka wa kumi na moja

"mpaka mwaka wa kumi na moja"

Jeremiah 52:6

Katika mwaka wa nne, siku ya tisa ya mwaka huo

Huu ni mwezi wa nne kwa kalenda ya Kiebrania. Siku ya tisa ni karibu na mwanzo wa Julai kwa kalenda ya Magharibi.

Mji

Huu ni mji wa Yerusalemu.

ulivunjwa

Watu wa Babeli waliubomoa ukuta uliozunguka mji.

kati ya kuta mbili

Hizi ni kuta mbili ukuta wa bustani ya mfalme na ukuta wa mji.

uwazi

"tambarare"

Jeremiah 52:9

Ribla

Huu ni mji.

mbele ya macho yake

"mbele yake"

Jeremiah 52:12

katika mwezi wa tano, siku ya kumi ya mwezi

Huu ni mwezi wa tano kwa kalenda ya Kiebrania. Siku ya kumi ni karibu na mwazo wa mwezi Agusti kwa kalenda ya Magharibi.

mwaka wa kumi na tisa

"katika mwaka wa kumi na tisa"

Nebuzaradani

Hili ni jina la mtu.

Walinzi

Hawa ni watu ambao kazi yao ni kumlinda mtu.

Jeremiah 52:15

Mafundi

Hawa ni watu ambao wanatengeneza vitu vizuri vinavyotumika katika kumuabudu Bwana.

Nebuzaradani

Hili ni jina la mtu.

watu masikini katika nchi

"watu masikini katika nchi"

Jeremiah 52:17

Bahari

Hivi ni vyombo vya maji vinavyotumika katika kumwabudu Bwana.

Jeremiah 52:20

Dhiraa

Dhiraa ni kipimo kinachotumika kupimia urefu au umbali.

Mashimo

Hii inamaanisha kuwa nguzo huwa na nafasi iliyowazi katikati.

Jeremiah 52:22

upande

Hii ni sehemu ya juu ya kila nguzo.

Jeremiah 52:24

Seraya

Hili ni jina la mtu.

Walinda lango

Mlinda lango ni mtu anayelinda katika lango.

uandaaji

"kujiandikisha" inamaana ya kwenda kwenye kazi.

Jeremiah 52:26

Nebuzaradani

Hili ni jina la mtu.

Ribla

Hili ni jina la mji.

Jeremiah 52:28

saba ... kumi na nane ... ishirini-tatu

7 ... 18 ... 20-3

Nebuzaradani

Hili ni jina la mtu.

3,023 ... 832 ...745 ... 4,600

elfu tatu na ishirini na tatu ... mia nane na thelathini na mbili ... mia saba na arobaini na tano ... elfu nne na mia sita.

Jeremiah 52:31

Katika mwaka wa thelathini na saba

mwaka wa saba

Katika mwezi wa kumi na mbili,siku ya ishirini na tano ya mwezi

Hii ni siku ya kumi na mbili na mwezi wa mwisho kwa kalenda ya Kienrania.

Ikawa

Neno hili limetumika kuonesha mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

Evil Merodaki

Alikuwa mfalme wa Babeli baada ya Nebukadreza.

Jeremiah 52:32

Aliongea nae kwa ukarimu

"Evil Merodaki aliongea na Yehoyakini"

kiti kilicho na heshima sana

"kiti ambacho meza yake ilikuwa karibu na kiti cha Evil Merodaki."

Lamentations 1

Lamentations 1:1

kama mjane

Haya maneno yana fananisha Yerusalemu na mwanamke asiye kuwa na ulinzi sababu mume wake amefariki.

Alikuwa mtoto wa mfalme miongoni mwa mataifa

"Matifa mengine yali heshimu Yerusalemu kama yalivyo muheshimu binti wa mfalme"

amelazimishwa utumwani

"amefanywa kuwa mtumwa"

Analia na kuomboleza

Mwanandishi anaelezea Yerusalemu kama mwanadamu mwenye hisia. Mji pia una wakilisha wakazi wake. "Wao wanao ishi humo wanalia na kuomboleza."

lia na kuomboleza

Neno "kuomboleza" lina husu sauti mtu anayo toa anapo "lia" kwa nguvu.

Lamentations 1:3

Yuda ameenda matekani

"watu wa Yuda wamepelekwa nchi ya kigeni"

hapati pumziko lolote.

"haoni pumziko" "ana wasiwasi tu"

Wanao wakimbiza wamewapata

"Wote walio kuwa wana mkimbiza wamefanikiwa kumkamata"

katika upweke wake

"alipo kuwa ana uwitaji"

Lamentations 1:4

Barabara za Sayuni zinaomboleza

Mwandishi anaelezea barabara zinazo elekea Sayuni zinaomboleza kama ni mwanadamu

sherehe iliyo andaliwa

"sherehe Mungu aliyo waambia wa shereheke"

Malango yake ... Makuhani wake

Neno "yake" na "wake" yaelezea Sayuni.

katika ugumu

"ana uchungu" au "ana kosa matumaini"

Maadui wake wamekuwa bwana zake

"Maadui wa Sayuni wana mtawala"

maadui wake wana fanikiwa

"maadui wake wanakuwa matajiri"

Yahweh

Hili ni jina la Mungu alilo lidhihirisha kwa watu wake katika Agano la Kale.

Lamentations 1:6

Uzuri umemwacha binti wa Sayuni

"Kila kitu kilicho kuwa kizuri cha binti wa Sayuni kimeharibiwa"

binti wa Sayuni

Hili ni jina

kama ayala ambaye haoni malisho

Watoto wa mfalme wanaliganishwa na swala asiye kuwa na kitu cha kula.

ayala

Ayale ni mnyama wa umbo la kati, anaye kula majani ambaye mara nyingi uwindwa na wanadamu. Pia ni mnyama mzuri wa kumtazama.

bila uwezo kwa

"lakini sio imara sana kukimbia kutoka"

wanao wakimbiza

"mtu anaye wakimbiza"

Lamentations 1:7

Katika siku za mateso yake na kutokuwa na nyumba

"Wakati Yerusalemu inapo kuwa inateswa na haina makazi"

hazina

"utajiri"

awali

"wakati uliyo pita" au "kabla ili janga halija tokea"

Wakati watu wake walipo angukia mikononi mwa adui

Hapa neno "mikononi" la husu jeshi la adui.

hakuna aliye msaidia

"hakuna msaidizi aliye kuwa naye"

waliwaona na kucheka maangamizo yake

Hii ina maana kuwa walikuwa na furaha na wakadhihaki Yerusalemu ilipo haribiwa.

maangamizo yake

"kwasababu aliharibiwa"

Lamentations 1:8

Yerusalemu ili tenda dhambi sana

Hii yaelezea Yerusalemu kama mtu aliye tenda dhambi, pia ina wakilisha wakazi wa Yerusalemu.

uchi wake

Yersualemu inaelezea kama mwanamke ambaye sehemu zake za siri zimefunuliwa kwa kila mtu amuaibishe.

Anguko lake lilikuwa baya

"Kuanguka kwake kulishangaza" au "hao walioyo muona

Angalia mateso yangu, Yahweh

Maana zinazo wezekana 1) mwandishi wa Maombolezo anaongea moja kwa moja na Yahweh au 2) Yerusalemu inaelezewa kuongea na Yahweh kama mtu.

Angalia

"kuwa makini"

Lamentations 1:10

ameeka mkono wake kwenye

"amechukuwa sehemu ya" au "ameiba"

hazina

utajiri

uliamuru

Hii ina maana kuwa mwandishi au mji bado unaongea, baada ya kuanza 1:8

Lamentations 1:11

hazina

"utajiri"

kurejesha uhai wao

"kuokoa uhai wao" au "kurejesha uweza wao"

Tazama, Yahweh, ni kumbuke mimi

Hapa Yerusalemu anaanza kuongea moja kwa moja na Yahweh.

Sio kitu kwako, wote mnao pita?

Hili ni shitaka la watu wanao pita Yerusalemu na hawaijali.

Sio kitu kwako

Hapa Yerusalemu anaendelea kuongea, lakini sasa kwa watu wanaopita.

Angalia na uone kama kuna mtu mwenye uzuni kama uzuni ninao teswa nao

Hii maana hapa inaelezea kuwa hakuna mtu aliye teseka kiasi hichi.

Angalia na uone

Haya maneno yana maana moja. Pamoja yana mkaribisha msomaji kuelewa kwa kuona kwamba hakuna mtu aliye teseka sana.

uzuni ninao teswa nao

"uzuni Yahweh anayo ni tesa nayo"

siku ya hasira yake kali

"Alipo kuwa na hasira kali"

Lamentations 1:13

alipo tuma moto kwenye mifupa yangu na umenishinda

"ametuma adhabu kali ndani yangu, na imeniharibu" au "ametuma adhabu mbaya katikati ya Yerusalemu, na imeharibu mji"

amenikabidhi mikononi mwao

"acha maadui zangu wanishinde"

Lamentations 1:15

wanaume wangu hodari walio niokoa

Katika hichi kipengele Yerusalemu bado yaelezewa kama mwanamke anaye jielezea.

wanaume hodari

"wanajeshi wenye nguvu"

kusanyiko

Hapa adui anaye shambulia Yerusalemu anaelezewa kama ni mkutano wa watu waliyo kuja pamoja ili kushitaki na kuhukumu.

wanaume imara

wanaume katika wakati kipindi chao cha nguvu

Bwana amewakanyaga ... chombo cha kusagia mvinyo

Hapa hukumu ya Mungu yaelezewa kama Yerusalemu ni mizabibu aliyo ikanyaga ili kukamua jwisi.

binti bikra wa Yuda

Hili ni jina la kishairi la Yerusalemu, mbapo hapa yaelezewa kama mwanamke. Neno "bikra" la hashiria kuwa mwanamke ni msafi.

Lamentations 1:16

ninalia

Hii bado ni Yerusalemu anaongea kama ni mwanamke, sasa ana hisia za uzuni.

Sayuni ametandaza mikono yake

Sayuni ni kama mtu anaye inua mikono yake kuomba msaada. Hapa Yerusalemu hajizungumzii yeye tena, lakini mwandishi anaelezea Yerusalemu.

hao karibu na Yakob

"watu karibu na Yakobo" au "mataifa yanayo zunguka Yakobo"

wawemaadui wake

Hapa neno "wake" la husu Yakobo.

Lamentations 1:18

nimeas

Hapa Yerusalemu anaanza kuzungumza tena, kama alikuwa mwanamke.

muone uzuni wangu

"ona jinsi gani nilivyo na majonzi"

Mabikra wangu na wanaume wangu hodari

"watu wangu wengi"

wanaume hodari

Ona jinsi ulivyo tafsiri 1:15

walikuwa na hila kwangu

"wali ni saliti"

kurejesha uhai wao

"kuokoa maisha yao" au "kurejesha uweza wao"

Lamentations 1:20

kwa kuwa nipo kwenye ugumu

Yerusalemu anaendelea kujizungumzia kama ni mwanamke, lakini sasa anazungumza moja kwa moja na Yahweh.

tumbo langu lina nguruma

Neno "nguruma" la maanisha kuangaika kwa nguvu, kawaida kwa mzunguko. Hii haimanishi kiuhalisia, lakini ndivyo linavyo jisikia.

moyo wangu umetibuka ndani yangu

"moyo wangu umevunjika" au "nina majonzi sana"

upanga umemliza

Upanga una husu adui, na "chukuwa" yamanisha "kuua" "adui anaua"

ndani ya nyumba kuna mauti tu

Maana inayo wezekana ni 1) katika nyumba, kila mtu ana kufa au 2) nyumba ni kama kaburi.

Lamentations 1:21

Wamesikia sononeko langu

Yerusalemu anaendelea kuongea kama mtu.

umenifanyia hivi

Hapa neno "wewe" la muhusu Yahweh.

Lamentations 2

Lamentations 2:1

Maelezo ya Jumla

Shairi lipya la anza. Mwandishi wa Maombolezo anatumia njia nyingi tofauti kuelezea kwamba watu wa Israeli wamepoteza upendeleo wa Mungu.

wingu la hasira yake

Maana inayo wezekana ni 1) Mungu anatishia kuwadhuru watu wa Yerusalemu au 2) Mungu tayari amesha wadhuru

binti wa Sayuni ... binti wa Yuda

Haya ni majina ya kishairi ya Yerusalemu, ambayo hapa yanazungumziwa kama ni mwanamke.

Ametupa utukufu wa Israeli chini kutoka mbinguni hadi duniani

"Yerusalemu amepoteza upendeleo wote na Bwana"

Hajakumba

"hajatilia maanani"

stuli yake

Hapa "stuli" ya wakilisha sehemu ambayo Mungu anaonyesha ukarimu wa kuwepo. Maana kadhaa hapa ni 1) "mji wake wa upendo Yerusalemu" au 2) "agano lake na Israeli."

siku ya hasira yake

kipindi cha wakati kwa ujumla, sio siku ya masaa 24

amemeza

"kaharibu kabisa" kama vile mnyama asivyo bakiza kitu anapo meza chakula

miji imara ya binti wa Yuda

Maana zinazo wezekana ni 1) miji yote imaraYuda nzima, au 2) kuta imara za Yerusalemu.

Lamentations 2:3

Maelezo ya Jumla

Mwandishi anaendelea kutumia mifano kuelezea upizani wa Mungu kwa Yuda.

amekata kila pembe ya Israeli

Hapa "pembe" (ambalo ni, pembe la mnyama) lina maana ya "uweza"

Ameurudisha mkono wake

"ameacha kutulinda na maadui zetu"

amepindisha upinde wake kuelekea kwetu

Mwanajeshi alipaswa kupindisha upinde wake ili kuupiga.

hema la binti wa Sayuni

"nyumba za watu Yerusalemu"

binti wa Sayuni

Kuna jina la kishairi la Yerusalemu, ambalo linazungumziwa hapa kama mwanamke.

Amemwaga gadhabu yake kama moto

"ameonyesha jinsi alivyo na hasira kwa kuwa haribu kila kitu kama mtu anavyo washa moto"

Lamentations 2:5

Amemeza

Ona jinsi ulivyo tafsiri 2:1

Ameongeza kilio na maombolezo

"Amesababisha zaidi na zaidi watu kulia na kuomboleza"

binti wa Yuda

Hili ni jina la kishairi la Yerusalemu, ambalo hapa la zungumziwa hapa kama mwanamke.

kajumba cha bustani

jengo dogo la kuhifadhia vifaa vya au kumuhifadhia mtu anaye tunza bustani

amesababisha kukusanyika na Sabato kusahaulika Sayuni

"amesababisha watu Sayuni kusahau kukusanyika na Sabato"

Lamentations 2:7

Ametoa ... mikononi mwa adui

"Ameugeuza kwa ... kwa adui"

Wamepaza sauti nyumbani mwa Yahweh, kama siku ya sherehe

Huu ni mfano wa kushangaza katika ya furaha, kelele za sherehe za Israeli na sauti za ushindi za wa Babilonia.

Lamentations 2:8

binti wa Sayuni

Hili ni jina la kishairi la Yerusalemu, ambalo la zungumziwa hapa kama mwanamke.

Amenyoosha kamba ya kipimo

"Amepima urefu wa ukuta" hivyo anajua kiasi cha kuharibu

hajauzuia mkono wake kutoharibu

"Ameharibu kwa kutumia nguvu zake zote"

hajauzuia mkono wake

"ameuweka mkono wake kwake"

Amefanya minara na ukuta kuomboleza; pamoja vilipotea

"Kwasababu ameharibu minara na kuta, inaonekana kama watu wanao omboleza na kupoteza nguvu"

Lamentations 2:10

binti wa Sayuni

Hili ni jina la kishairi la Yerusalemu, ambalo la zungumziwa hapa kama mwanamke.

keti chini

kuonyesha walikuwa wana omboleza

Lamentations 2:11

Maelezo ya Jumla

Mwandishi anatoka kuelezea Yerusalemu na kueleza mapito yake.

Macho yangu yamekaukiwa machozi yake

"Nimelia hadi siwezi kulia tena"

sehemu zangu za ndani zimemwagika chini

"sehemu yangu ya ndani ipo katika uzuni"

kwasababu ya uharibifu wa binti wa watu wangu

"binti wa watu wangu" ni jina la kishairi la Yerusalemu,ambalo hapa la zungumziwa kama mwanamke.

Mbegu ziko wapi na mvinyo?

Maneno "mbegu ba mvinyo" ni namna ya kusema "chakula na kinywaji."

Lamentations 2:13

Maelezo ya Jumla

Mwandishi anaanza kwa kusema na Yerusalemu.

Nini naeza kusema ... Yerusalemu?

"Hakuna nacho weza kusema ... Yerusalemu."

binti wa Yerusalemu

Hili ni jina la kishairi la Yerusalemu, ambalo hapa la zungumziwa kama ni mwanamke.

Naweza kufananisha na nini ... Sayuni?

"Hakuna nachoweza kukufananisha nacho ... Sayuni."

Nani anaweza kukuponya?

"Hakuna anaye weza kukuponya"

Lamentations 2:15

wana piga makofi

namna ambazo watu wana wa tania wengine na kuwa tusi

binti wa Yerusalemu

Hili ni jina la kishairi la Yerusalemu, ambalo hapa la zungumziwa kama ni mwanamke.

Huu ndio mji walio uita 'Ukamilifu wa uzuri,' ''?

Hili ni swali linalo tumika kueleza kejeli." Huu mji walio uwita 'Ukamilifu wa uzuri,' 'Furaha ya Dunia Yote' sio mzuri wala wafuraha tena!"

Tumemmeza yeye

"Tumeharibu Yerusalemu kabisa" kama mnyama anavyo meza chakula

Lamentations 2:17

menyanyua pembe za maadui zako

Hapa "pembe" (kwamba ni, pembe ya mnyama) mara nyingi yaelezea uweza.

Lamentations 2:18

Mioyo yao ikamlilia

Maana inayo wezekana ni 1) "Watu wa Yerusalemu wamepiga kelele kutoka kwenye vilindi vyao" au 2) mwandishi anataka kuta zipaze sauti kwa Yahweh.

kuta za binti wa Sayuni ... kila mtaa

Mwandishi anaongea na kuta za Yerusalemu. Anataka watu wa Yerusalemu kufanya anacho ambia kuta zifanye.

binti wa Sayuni

Hili ni jina la kishairi la Yerusalemu, ambalo hapa la zungumziwa kama ni mwanamke.

Fanya machozi yako kutiririka chini kama mto

"kulia machozi mengi"

usiku na mchana

"wakati wote"

Usijipatie hauweni

"Usijiruhusu upumzike"

mwanzo usiku wa manane

"mara nyingi wakati wa usiku" hiyo ni kwamba, mlinzi anapo kuja kulinda

Nyoosha juu mikono yako

Hili ni tendo linalo fanywa wakati wakuomba.

kwenye njia ya kila mtaa

"pale njia zinapo kutana" au "kwa barabarani"

Lamentations 2:20

Wanawake wale tunda la uzazi wao ... wajali?

"Wanawake wasiwale watoto wao ... wajali?

tunda la uzazi wao

"watoto walio bado wadogo"

Lamentations 2:21

wadogo kwa wakubwa

wadhaifu na watu wazima wenye nguvu

hofu yangu

"washambuliaji niliyo kuwa nawaogopa"

kama ungewaita watu katika siku ya maakuli

"kama wange kuwa wanakuja kwenye sherehe"

Lamentations 3

Lamentations 3:1

Sentesi Unganishi

Shairi lipya laanza

chini ya gongo la hasira ya Yahweh

Ngongo ni fimbo watu waliyo tumia kupiga na kuadhibu mtu.

kutembea kwenye giza kuliko kwenye nuru

Hii ina maanisha kuishi kwenye kuchanganyikiwa pamoja na giza.

amenigeuzia mkono wake dhidi yangu

"amekuwa adui wangu" au "anatumia nguvu yake kunihukumu"

Lamentations 3:5

Amejenga vifusi vya udogo dhidi yangu

Vifusi vya udogo vina muwezesha jeshi shambulizi kuvuka kuta na kuvamia mji.

kunizingira na uchungu na ugumu

"kanizunguka na vitu vilivyo na maumivu na vigumu kuvumilia"

anazima maombi yangu

"anakataa kusikiliza maombi yangu"

Lamentations 3:9

Ameziba njia yangu

"alinizuia kuto mtoroka"

mawe ya kuchonga

mawe mtu aliyo yakata katika maumbo yakulingana yanayo ingiliana na kuimarisha ukuta

mawe; amefanya njia yangu mbaya

Maana inayo wezekana ni 1) "mawe, hivyo siwezi kwenda sehemu" au 2) "mawe; kila njia ninayo ichukuwa haiende mahali"

amegeuza pembeni njia zangu

Maana inayo wezekana ni 1) "amenivuta nje ya njia" au 2) "kasababisha njia yangu kwenda kumelekeo mbaya"

Lamentations 3:12

Amepindisha upinde wake

Ona jinsi ulivyo tafsiri 2:3

maini

viungo vya tumbo linalo peleka mkojo kwenye kibofu.

kichekesho kwa watu wangu wote

Maana inayo wezekana ni 1) "mtu ambaye Israeli yote yamcheka" au 2) "mtu ambaye watu wote wa dunia wanamcheka"

Amenijaza kwa uchungu

"Ni kama kanilazimisha nile mimea michungu"

maji machungu

jwisi chungu kutoka kwenye majani na maua ya mimea

Lamentations 3:16

Alivunja ... amenisukuma

ni maneno mawili Mungu anayo mnyenyekesha mwandishi

Nafsi yangu imenyimwa amani

Mwandishi pitii tena furaha au starehe kwenye maisha yake.

Ustahimilivu wangu umeangamia

"Tafsiri zingine zinasema, "Utukufu wangu umeangamia," lakini hapa "utukufu" una maana ya uvumilivu au uweza.

Lamentations 3:19

nimeinama ndani yangu

Haya maelezo yana hashiria msongamano wa mawazo na kukosa tumaini.

Lakini ni vuta hili akilini mwangu

Mwandishi anataka kuwambia wasomaji ni anatumainia.

Lamentations 3:22

uaminifu wako

Mwandishi anazungumza na Yahweh.

Yahweh ni urithi wangu

"Kwasababu Yahweh yupo nami, nina kila kitu ninacho kiitaji"

Lamentations 3:25

wanao msubiri

Maana inayo wezekana ni 1) "wote wanao mtumainia" (UDB) au 2) "yeye anaye msubiri kwa uvumilivu kutenda."

anaye mtafuta

"mtu anaye mtafuta"

kubeba nira

"kuteseka"

imewekwa juu yake

"nira imewekwa juu yake"

aeke mdomo wake kwenye vumbi

"kuinama chini na mdomo kwenye ardhi"

Lamentations 3:30

Maelezo ya Jumla

Mwandishi anaongea juu ya yeye anaye msubiri Yahweh 3:25

Acha atoa shavu lake kwa yeye anaye mpiga

"Acha aruhusu watu wampige"

japo anatia

"japo Yahweh anasababisha"

watoto wa mwanadamu

"wanadamu" au "watu"

Lamentations 3:34

Kukanyaga chini ya mguu

"Kumtumia vibaya" au "Kumuua"

Lamentations 3:37

Sio kutoka mdomoni mwa Aliye Juu majanga na mazuri yanakuja?

"Mungu anapunguza mahafa au mafanikio kwa kila mtu"

Lamentations 3:40

Na tunyanyue mioyo yetu na mikono yetu

Ili kuwa ni utamaduni wa Waisraeli kunyoosha mikono yao wakiomba kwa Mungu.

Tumekosea na kuasi

Maneno "kosea" na "kuasi" yanashiriki maana moja. Pamoja yana hashiria kuwa makosa ni sawa na kuasi dhidi ya Yahweh.

Umejifunika na hasira

Hapa hasira inazungumziwa kama ni vazi Mungu alilo livaa. Kiebrania mara nyingi cha ongelea hisia kama vile ni nguo.

Lamentations 3:44

Maelezo ya Jumla

Maombi yaliyo anza 3:40 yanaendelea.

Umejifunika na wingu ili kwamba kusiwe na ombi linaloweza kupita

"Unatumia mawingu kama ngao kuzuia maombi yetu"

Umetufanya kama uchafu na taka miongoni mwa mataifa

Maneno "uchafu" na "tak" yote ya husu vitu watu walivyo vikataa na kuvitupa.

miongoni mwa mataifa

Maana inayo wezekana ni 1) mataifa mengine yana onekana kama taka taka (UDB), au 2) kwamba Yahweh ametupa kama uchafu miongoni mwa mataifa.

maafa na uharibifu

Haya maneno mawili yana shiriki maana moja na ya husu uharibifu wa Yerusalemu.

Lamentations 3:48

Macho yangu yanatiririka na miferiji ya machozi

"Machozi yana tiririka kutoka machoni mwangu kama maji yanavyo tiririka mtoni" kwasababu nalia

kwasababu ya watu wangu

Ona jinsi ulivyo tafsiri 2:11

Lamentations 3:51

Macho yangu yana ni sababishia uzuni

"Ninacho kiona kina ni sababisha maumivu"

mabinti wa mji wangu

Maana inayo wezekana ni 1) wanawake wa Yerusalemu au 2) wakazi wote wa Yerusalemu.

Wamenitupa kwenye shimo

"Wameniua kwa kunizamisha kwenye kisima"

wakanitupia jiwe

Maana inayo wezekana ni 1) "wametupa mawe" au 2) "wamefunika kisima kwa jiwe."

Nimekatwa mbali

"Nimeuawa" au "Nimezama"

Lamentations 3:55

Nililiita jna lako

"Nilikuita kwa ajili ya msaada"

kutoka kina cha shimo

Maana inayo wezekana ni 1) "kutoka kisima kirefu" au 2) "kutoka kaburini"

Ulisikia sauti yangu

"Ulisikia nilicho kisema"

Usifunge sikio lako

"Usikatae kunisikia"

Lamentations 3:58

ulitetea kesi yangu

Hii yatoa picha ya mahakama, ambapo mwandishi anashitakiwa. Katika hii picha, Mungu anamtetea, kama wakili anavyo mtetea mteja wake.

hukumu kesi yangu

Hapa Mungu haendelei kuonekana kwenye picha kama wakili, lakini kama mtoa hukumu.

matusi yao, mipango yao yote dhidi yangu

Hii mistari miwili ina shiriki maana moja na imewekwa pamoja kwa mkazo.

Umesikia dhihaka yao

"Umesikia wakinikejeli"

Lamentations 3:62

Midomo ya hao wanao inuka kinyume changu

"Maneno hao walio inuka dhidi yangu wamenena"

hao wanao inuka kinyume changu

"hao wanao nishambulia"

jinsi wanavyo keti na kuinuka

"kila wanacho fanya"

Lamentations 3:64

Walipize, Yahweh, kwa kadiri ya waliyo fanya

"Wamenifanya ni teseke, Yahweh, hivyo tafadhali wafanye wateseka sasa"

taacha mioyo yao bila lawama

"wasabishe wa sijisikie aibu"

nchini ya mbingu

"popote walipo duniani"

Lamentations 4

Lamentations 4:1

Maelezo ya Jumla

Shairi lipya la anza.

Mawe matakatifu

mawe yaliyo unda hekalu

katika kila njia ya mtaa

Ona jinsi ulivyo tafsiri 2:18

Wana wa Sayuni

Maana inayo wezekana ni 1) Wanaume wadogo wa Yerusalemu au 2) watu wote wa Yerusalemu.

lakini sasa hawana thamani zaidi ya majagi ya udogo, kazi ya mikono ya mfinyazi!

"watu wali wachukulia kuwa si kitu kama vishungu vya udogo wafinyazi wanavyo tengeneza!"

Lamentations 4:3

mbwa wa mitaani wanatoa maziwa yao kuwanyonyesha watoto wao

Hii ina maana kuwa mbwa wa mitaani wa kike kwa uhuru wanaruhusu watoto wao kunyonya.

mbwa wa mitaani

mbwa wa kali, wa katili wa wanyama wa chafu

binti wa watu wangu

Hili ni jina la kishairi la Yerusalemu, ambalo hapa la zungumziwa kama ni mwanamke. Ona jinsi ulivyo tafsiri 2:11

Lamentations 4:4

wao walio lelewa kwa kuvaa nguo za zambarau

Kuvaa nguo rangi ili hashiria mtu ana utajiri.

Lamentations 4:6

Hukumu

Maana inayo wezekana ni 1) "adhabu kwa dhambi" au 2) "dhambi."

binti wa watu wangu

Hili ni jina la kishairi la Yerusalemu, ambalo linazungumziwa hapa kama ni mwanamke.

ilipinduliwa kwa dakika

"Mungu alimuonyesha kwa dakika"

hakuna aliye yanyua mkono kumsaidia

"japo hakuna mtu aliyw msaidia"

Lamentations 4:7

Viongozi wake walikuwa wasafi kuliko theluji

Maana inayo wezekana; 1) "Viongozi wetu walikuwa wazuri kutazama awali" (UDB) kwasababu walikuwa wenye afya kimwili au 2) watu waliwapenda viongozi wao kwasababu viongozi walikuwa wasafi kimatendo jinsi theluji na maziwa yalivyo meupe.

Viongozi wake

Viongozi wa Yerusalemu

yakuti samawi

jiwe la gharama linalo tumika kwenye mikufu

Muonekano wao umekuwa mweusi kama giza

Hii ya weza maanisha 1) jua limefanya ngozi za viongozi kuwa nyeusi au 2) moshi kutoka kwenye moto ulio choma Yerusalemu umefunika nyuso zao.

hawatambuliki

"Hakuna anaye weza kuwatambua"

imekuwa kavu kama kuni

kwasababu hawana chakula cha kutosha na maji

Lamentations 4:9

Hao walio uawa kwa upanga

"Hao wanajeshi maadui waliyo waua

hao walio kufa kwa njaa

"hao walio umwa na njaa hadi mauti"

walio potea

"hao waliyo kuwa wembamba na wadhaifu kwasababu walikuwa wana kufa kwa njaa"

wakatobolewa kwa ukosefu wa mavuno shambani

Ukosefu wa chakula unazungumziwa hapa kama ni upanga.

Mikono ya wanawake wenye huruma

"wanawake wenye huruma"

Lamentations 4:11

Yahweh alionyesha gadhabu yake yote; alimwaga hasira yake kali

Yahweh alikuwa na hasira sana, na amefanya kila kitu alichotaka kufanya kuonyesha alikuwa na hasira.

alimwaga hasira yake kali

Hasira ya Mungu ni kama moto, maji ya moto anayo mwaga.

Aliwasha moto Sayuni

Hii inaweza maanisha 1) hasira ya Mungu ni kama moto uliyo haribu Yerusalemu, au 2) kwamba Mungu alisababisha maadui wa chome Yerusalemu kwa moto.

Lamentations 4:12

Wafalme wa dunia hawaku amini, wala wakazi wa dunia,

"Hakuna mtu popote aliye amini"

maadui au wapinzani

Haya maneno mawili yana maana moja na yanakazia kuwa hawa ni watu waliyo waliyo tamani kudhuru Yerusalemu.

dhambi za manabii na maasi ya makuhani

Hii mistari miwili ina maanisha kitu kimoja na kukazia kuwa hawa viongozi wa kiroho walikuwa wanahusika na kuanguka kwa Yerusalemu.

walio mwaga damu ya wenye haki

Wote makuhani na manabii walikuwa na hatia ya mauaji.

Lamentations 4:14

Walikuwa wamejitia unajisi kwa damu hiyo

Kwasababu wameshiriki mauaji, hawana usafi, wasio weza kumtumikia Mungu au kuwa na watu wa kawaida.

Lamentations 4:16

akawatawanyisha

akawatawanyisha makuhani na manabii

hawatazami tena

"haendelei kuwa kubali tena" au "haendelei kuwa idhinisha tena"

Lamentations 4:17

Macho yetu yalikwama

Maana inayo wezekana ni 1) walitafuta watu wawasaidie, lakini hakuna msaada uliyo kuja au 2) waliendelea kutafuta masaada kutoka kwa watu wasingeweza kuwa saidia.

Walifuata hatua zetu

"Maadui zetu waliwafuta kila sehemu walipo enda"

mwisho wetu

"Wakati wa sisi kufa"

Lamentations 4:19

Pumzi katika pua zetu

Hii ni cheo cha mfalme, anaye toa uzima kwa watu wake kama pumzi inavyo upa mwili uhai.

aliye kamatwa katika shimo

Hapa "shimo" la husu mtego wa adui, mpango wao wa kumkamata adui.

Lamentations 4:21

Shangilia na ufurahi

Haya maneno mawili yana maana moja na yana kazia uzito wa furaha. Mwandishi anatumia haya maneno kwa kejeli.

Binti wa Sayuni ... binti wa Edomu

Haya ni majina ya kishairi ya watu wa Yerusalemu na nchi ya Edomu, ambapo hapa yana zungumziwa kama mwanamke.

kwako pia kikombe kitapitishwa

Mvinyo watu wanao kunywa kutoka kwenye kikombe ni hishara ya hasira ya Yahweh.

ata funua dhambi zako

"kuweka wazi dhambi zako"

Lamentations 5

Lamentations 5:1

Maelezo ya Jumla

Shairi lipya la anzu.

Kumbuka

"Fikiria kuhusu"

uone aibu yetu

"angalia hali ya aibu tuliyo nayo"

Urithi wetu umegeuziwa kwa wageni

"Umeruhusu wageni kuchukua "

nyumba zetu kwa wageni

"umeruhusu wageni wachukuwe mali za urithi wetu"

Tumekuwa yatima ... mama zetu ni kama wajane

Watu wa Yerusalemu hawana mtu wa kuwalinda kwasababu wanaume wamekufa vitani au wameenda matekani.

Lazima tulipe fedha kwa maji tunayo kunywa

"Lazima tulipe fedha kwa maadui zetu ili tunywe maji yetu"

tulipe fedha kupata mbao zetu

"maadui zetu wanatuuzia mbao zetu"

Lamentations 5:5

Hao wanakuja kwetu

Jeshi la wa Babilonia.

Tumejitoa kwa

"tumefanya maridhiano na" au "tumejisalimisha kwa"

tupate chakula cha kutosha

"ili tuwe na chakula cha kutosha kula"

hawapo tena

"wamekufa"

tumebeba dhambi zao

"tunabeba adhabu ya dhambi zao"

Lamentations 5:8

Watumwa walitutawala

Maana inayo wezekana ni 1) "Sasa watu wanao tutawala wao wenyewe ni watumwa kwa mabwana zao Babilonia" (UDB) au 2) "Watu walikuwa watumwa Babilonia wanatutawala."

kutuokoa na mikono yao

Hapa neno "mkono" la husu nguvu.

kwasababu ya upanga wa nyikani

"kwasababu kuna watu nyikani wanao ua watu kwa upanga"

Lamentations 5:11

Wanawake wanabakwa Sayuni ... mabikra katika mji wa Yuda

"Wanawake wote, wadogo na wakubwa, wanabakwa Yerusalemu na miji ya Yuda"

Watoto wa mfalme wamenyongwa na mikono yao

Maana inayo wezekana ni 1) "Kwa mikono yao, wamenyonga watoto wa wafalme" au 2) wamefunga mikono ya watoto wa wafalme pamoja kwa kama ili miguu yao isiguse chini.

Lamentations 5:13

Wazee

wanaume wasio na "nguvu" tena

lango la mji

sehemu wazee wangetoa mashauri, lakini pia sehemu watu wange kutana

miziki

sehemu ya sanaa katika lango la mji

Lamentations 5:15

Taji limeanguka kichwani mwetu

Maana inayo wezekana ni 1) "Sisi hatuvai tena maua kichwani mwetu kwa ajili ya sherehe" au 2) "Hatuna tena mfalme"

Lamentations 5:17

macho yetu yanafifia

"tuna ona kwa shida kwasababu ya machozi yetu"

mbwa wa mitaani

Ona jinsi ulivyo tafsiri 4:3. Sehemu zilizo haribiwa zilikuwa zimevamiwa na mbwa hawa wa mitaani, pamoja na wengineo.

Lamentations 5:19

kiti chako cha enzi

"nguvu yako na mamlaka ya kutawala kama mfalme"

vizazi na vizazi

"wakati wote"

Kwanini unatusahau milele? Kwanini unatutelekeza kwa siku nyingi?

"ni kama vile utatusahau milele au usiturudie kwa kipindi kirefu"

Fanya upya siku zetu kama zilivyo kuwa hapo zamani

"Fanya maisha yetu mazuri, kama yalivyo kuwa" au "Fanya tuwe wakuu kama tulivyo kuwa"

vinginevyo labda uwe umetukataa na una hasira kwetu kupita kiasi

Maana inayo wezekana ni 1) mwandishi ana ogopa kwamba Yahweh anaweza kuwa na hasira asiwarejeshe au 2) anasema kuwa Yahweh ana hasira hadi hawezi kuwarejesha (UDB)

Ezekiel 1

Ezekiel 1:1

Katika mwaka wa kumi na tatu

Huu ni mwaka wa kumi na tatu ya uhai ya Ezekieli.

mwezi wa nne, na siku ya siku ya tano ya mwezi

"siku ya tano ya mwezi wa tano." Huu ni mwezi wa nne wa kalenda ya Kiebrania. Siku ya tano inakaribia mwishoni mwa mwezi wa sita kwenye kalenda za Magharibi.

Ikawa kwamba

Hili neno limetumika hapa kuonyesha tukio muhimu katika hadithi.

Nilikuwa nikiishi miongoni mwa mateka

Neno "Mimi" inamrejelea Ezekieli. "Nilikuwa miongoni mwa mateka"

Nikaona maono ya Mungu

"Mungu alinionyesha mambo yasiyo ya kawaida"

ilikuwa mwaka wa tano wa uhamisho wa Mfalme Yehoyakini

Kupitia hiki kitabu, Ezekieli ataandika tarehe juu ya lini Wababeli waliwalazimisha Yehoyakini kuondoka Yerusalemu.

kwa Ezekieli ... juu yake huko

Ezekieli anajizungumzia yeye mwenyewe kana kwamba alikuwa mtu mwingine.

neno la Yahwe lika kwa nguvu kwa Ezekieli

"Yahwe alinena kwa nguvu na Ezekieli"

Buzi

jina la kiume

Keberi Kanali

Huu ni mto ambao watu katika Kaldea walichimba kupeleka maji kwenye bustani zao. "Mto Keberi"

mkono wa Yahwe ulikuwa juu yake

Neno "mkono" mara nyingi limetumika kurejelea nguvu ya mtu au tendo.

Yahwe

Hili ni jina la Mngu ambaye aliyejifunua kwa watu wake katika Agano la Kale.

Ezekiel 1:4

Sentensi Unganishi:

Ezekieli anaendelea kuelezea ono lake.

upepo wa dhoruba

Hii ni dhoruba ambayo yenye upepo mwingi.

unakuja kutoka kaskazini

Kaskazini ni uelekeo wa mkono wako wakati utazamapo jua linapokuwa linachomoza.

wingu kubwa lenye moto ndani yake

Hili linaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya: "Hii dhoruba ilikuwa kubwa pamoja na moto ukiwaka ndani yake"

moto ukiwaka

Maana ziwezekanazo 1) "mwanga ukiwaka" au 2) ukiwaka wakati wote."

na nuru ndani yake na kung'aa ukizunguka ndani yake

"na nuru kali sana ikimulika ilikuwa imelizunguka wingu ndani yake".

rangi ya kaharabu

"njano inayong'aa kama kaharabu" au "njano inayong'aa"

kaharabu

utomvu wa njano ngumu ambayo ilitumika kama pambo zuri juu ya kito

Katikati

"katikati ya dhoruba"

ulikuwa kama mwonekano wa viumbe hai vinne

"kulikuwa na vitu ambavyo vilifanana kama viumbe vinne"

Huu ulikuwa mwonekano wao

"Hivi ndivyo ambayo viumbe vinne vilivyokuwa vikionekana"

vilikuwa vikifanana na mtu

"vile viumbe vinne vilifanana na watu"

lakini vilikuwa na sura nne kila mmoja, na kila kiumbe kilikuwa na mabawa manne

"lakini kila kiumbe kilikuwa na sura tofauti tofauti na mabawa manne." Kila kiumbe kilikuwa na uso mmoja kwa mbele, uso mmoja upande wa nyuma, na uso mmoja kwa kila upande wa kichwa chake.

Ezekiel 1:7

Sentensi Unganishi:

Ezekieli anaendelea kueleza ono lake.

lakini nyao za miguu yao zilikuwa kama kwato za ndama

"lakini miguu yao ilionekana kama kwato za ndama"

kwato za ndama

sehemu ngumu ya mguu wa ndama

zilizokuwa zinang'aa kama shaba iliyosuguliwa

"zilizokuwa zimeng'aa kama shaba ambayo iliyokuwa imeoshwa." Hii inaelezea miguu ya viumbe.

juu ya pande zote nne

"juu ya pande zote nne za miili yao"

Kwa zote nne, nyuso zao na mabawa zilikuwa kama hivi"

"Kwa viumbe vyote vinne, mabawa yao na nyuso zao zilikuwa kama hivi"

na hawakugeuka walipokuwa wakienda

"na viumbe havikugeuka vilipokuwa vikitembea"

Ezekiel 1:10

Sentensi Unganisha:

Ezekieli anaendelea kuelezea maono yake

Mwonekano wa nyuso zao zilikuwa kama uso wa mwanadamu

Ezekieli anaelezea nyuso za hao viumbe kwa upande wa mbele. "Nyuso za kila kiumbe zilionekana kama hivi: Mbele ya uso palionekana kama uso wa mwanadamu"

uso wa simba kwa upande wa kuume

"kwa upande wa kulia wa kichwa chake palionekana kama uso wa simba"

"uso ulikuwa wa maksai uapnde wa kushoto

"upande wa kushoto wa uso wa kichwa ulikuwa unafanana na uso maksai"

mwishoni, uso wa tai

"mwishoni, uso wa upande wa nyuma wa kichwa chake ulifanana kama uso wa tai"

mabawa yao yalikuwa yametawanyika juu, hivyo basi kila kiumbe kilikuwa na jozi ya za mabawa yaliyokuwa yameshikamana na bawa la kiumbe kingine

"kila kiumbe kilishikilia mabawa yake mawili ili bawa moja liligusa bawa la kiumbe upande mwingine wa kiumbe kingine, na bawa jingine liligusa kiumbe kwa upande mwingine wa kiumbe kingine"

na pia njozi ya mabawa iliyokuwa imefunika miili yao

"Mabawa mengine mawili ya kila kiumbe yalifunika mwili wake"

Kila mmoja alienda mbele

"Kila kiumbe kilienda na uso ukiwa umetazama mbele"

Ezekiel 1:13

Sentensi Unganishi:

Ezekieli anaendelea kuelezea maono yake.

ulifanana kama mkaa uliochomwa, au kama tochi

"uling'aa kama mkaa katika moto mkali, au kama tochi"

na kulikuwa na tochi imewaka

"na mwanga ulikuja kutoka kwenye moto."

Hao viumbe hai vilikuwa vikihama mbio mbele na nyuma, na walikuwa na mwonekano wa radi

Tochi zilizowaka na kupotea upesi, na viumbe walienda kutoka upande mmoja kwenda mwingine upesi.

Ezekiel 1:15

Sentensi Unganishi:

Ezekieli anaendelea kuelezea maono yake.

kulikuwa na gurudumu moja juu ya nchi karibu na viumbe hai

"kulikuwa na gurudumu moja juu ya nchi karibu na kila mmoja wa viumbe hai, gurudumu moja kwa kila mweliekeo viumbe walipokuwa wameelekea"

Huu ndio ulikuwa mwonekano na umbo wa hizo gurudumu

"Hivi ndivyo magurudumu yalivyofanana na jinsi yavyokuwa yametengenezwa"

kama zabarajadi

Zabarajadi ni aina ya weupe, jiwe la thamani, mara nyingi la njano au rangi ya dhahabu."jeupe na manjano kama jiwe la zabarajadi"

hayo manne yote yalikuwa sawa sawa

"yote manne ya magurudumu yalifanana"

walifanana kama gurudumu linalofanana na jingine

"yalitengenezwa na gurudumu moja linaloenda kupitia gurudumu jingine"

Ezekiel 1:17

Sentensi Unganishi:

Ezekieli anaendelea kulezea maona yake

walienda bila kugeuka mahali popote viumbe walipokuwa wameelekea

"magurudumu yalikuwa yanaweza kwenda katika mahali popote penye njia nne ambapo viumbe walipokuwa wameelekea"

Kama kwa ajili ya kingo zao

"Hivi ndivyo kingo za magurudumu zilifanana"

walikuwa warefu na wakutisha

"kingo zilikuwa ndefu na zakutisha"

kingo zikuwa zimejaa macho yaliyozunguka

"kwa sababu kingo zilikuwa zilikuwa nyingi sana kuzunguka magurudumu yote manne"

Ezekiel 1:19

Wakati viumbe hai walipoinuka kutoka kwenye nchi

Viumbe vilikuwa vikiruka katika anga baada kuondoka kwenye nchi. "Hivyo wakati viumbe walipoicha nchi na kwenda juu kwenye anga."

roho wa kiumbe hai

"roho yule yule aliyetoa uhai kwa viumbe pia alitoa uhai kwa magurudumu."

magurudumu pia yaliiuka

"magurudumu pia yaliiacha nchi na kwenda kwenye anga"

Popote Roho alipoenda, walienda

Neno "wao" hurejelea kwa viumbe.

magurudumu waliinuka juu karibu nao

"magurudumu yalipanda juu kwenye anga pamoja na viumbe hai"

Ezekiel 1:22

anga itanukayo

Kuba huonekana kama mpira mtupu uliokatwa nusu. "Kutanuka" maana yake kubwa sana.

fuwele inayovutia

fuwele inayovutia- "barafu inayong'aa"

yaliyonyooshwa kuelekea juu ya vichwa vyao

"na kuba inayotanuka ilikuwa imesambazwa juu ya vichwa vya viumbe"

Benethi kuba

"chini ya kuba"

Kila viumbe hai pia vilikuwa na njozi moja kujifunika wenyewe; kila kiumbe kilikuwa na njozi moja kufunika mwili wake mwenyewe

"Kila viumbe hai pia vilikuwa na mabawa mawili mengine, ambavyo walitumia kufunika miili ya"

Ezekiel 1:24

Maelezo ya Jumla:

Ezekieli anaendelea kueleza kuhusu maono ya viumbe hai.

Kisha nikasikia sauti ya mabawa yao. Kama mlio wa maji mengi. Kama sauti ya mwenye enzi popote walipoelekea. Kama

"Popote walipoelekea, nalisikia sauti ya mabawa yao. Kama sauti ya maji yanayoruka.

Kama ... maji. Kama ... tembea. Kama ... dhoruba ya mvua. Kama ... jeshi

Hizi sentensi hazijakamilika kwa sababu Ezekieli alikuwa akionyesha kwamba alikuwa na furaha kubwa kuhusu alichokiona. "Mabawa yalisikika kama ... maji. Yalisikika kama ... tembea. Yalisikika kama ... dhoruba ya mvua. Yalisikika ... jeshi."

maji yaliyotibuka

Hii inamaana rahisi "maji mengi." Ingeweza kurejelewa kwa "mto wenye sauti kubwa"

Kama sauti ya enzi

Wakati mwingine Biblia inarejea radi kama "sauti ya enzi." "Ilisikika kama sauti ya mwenyezi Mungu"

Kama sauti ya dhoruba ya mvua

"Kama sauti ya dhoruba kubwa sana"

Popote waliposimama

"Popote viumbe walipoacha kutembea"

walishusha mabawa yao

"hao viumbe waliacha mabawa yao kuning'ining'a chini karibu na sehemu zao." Walifanya hivyo wakati walipoacha kutumia mabawa yao kuruka.

Sauti ikaja kutoka juu ya anga

"Mtu aliyekuwa juu ya anga akinena." Kama unahitaji kueleza sauti hii ni ya nani, unaweza kujaribu kuitambua kama sauti ya Yahwe

anga juu ya vichwa vyao

"anga lililokuwa juu ya vichwa vya viumbe"

anga

huonekana kama mpira mtupu uliokatwa juu na chini.

Ezekiel 1:26

juu ya vichwa

"juu ya vichwa vya viumbe hai"

ulikuwa na mwonekano wa kiti cha enzi

"kulikuwa na kitu kilichofanana kama kiti cha enzi"

samawati

jiwe la thamani sana ambalo ni blu safi na ling'aalo sana

juu ya kiti cha enzi kulikuwa

"juu ya kiti cha enzi kulikuwa"

mwonekano wa mmoja aliyefanana kama mwanadamu

"mtu aliyefanana na mwanadamu"

Ezekiel 1:27

Maelezo ya Jumla:

Ezekieli anaendelea kueleza kuhusu maono.

kutoka kwenye nyonga juu

Mwili wa mwanadamu juu ya nyonga palifanana kama chuma kinachong'aa kilichokuwa na moto ndani mwake.

kuzunguka kote

"kuzunguka kote mtu aliyeketi juu ya kiti cha enzi"

kutoka kwenye nyonga kwa chini palionekana kama moto na mng'ao ulozunguka kote

"Kumzunguka kote chini ya nyonga, niliona kilichofanana kama moto na mwanga ung'aao."

Ilionekana kama upinde wa mvua unaoonekana katika mawingu katika siku ya mvua, na kama mwanga unaong'aa ukiizunguka

"Mwanga ambao ulikuwa umemzunguka kote ulifanana kama upinde wa mvua uonekanao katika mawingu katika siku ya mvua inyeshapo."

upinde wa mvua

rangi nzuri ya mustari wa mwanga uonekanao katika mvua wakati jua liwakapo kutoka nyuma ya mwonekano

Huu ulionekana kama mfanano wa utukufu wa Yahwe

"Mwanga unaong'aa ulifanana kama kitu ambacho kilichofanana na utukufu wa Yahwe."

niliusikia kwenye uso wangu

"nilisujudu hata chini kwenye nchi" Ezekieli hakuanguka kwa ajali. Alienda chini hata kwenye nchi kuonyesha kwamba aliheshimu na kumwogopa Yahwe.

nilisikia sauti ikinena

Neno "sauti" ni picha ya mtu. "nikasikia sauti ikinena"

Ezekiel 2

Ezekiel 2:1

Maelezo ya Jumla:

Ezekieli anaendelea kueleza kuhusu maono aliyoyaona.

Akanambia

"yule aliyefanana na mwanadamu". (1:2). Hakuwa "yule Roho."

ROho

"roho" au "upepo."

Mwana wa mtu

"Mwana wa mwanadamu" au "Mwana wa binadamu." Mungu anamuita Ezekieli hivi kusisitiza kwamba Ezekieli ni mwanadamu tu. Mungu ananguvu na huishi milele, lakini watu hawawezi. "utu wa kufa" au "Binadamu"

kwa watu wa Israeli, kwa taifa lililo asi

"kwa Waisraeli, kwa watu walioasi." Manano haya mawili huwarejea watu wale wale. "kwa watu wa Israeli, ambao ni waasi."

hata hivi leo

Hii inamaanisha kwamba watu wa Israeli waliendelea kutokumtii Mungu. "hata sasa" au "hata leo."

Ezekiel 2:4

Maelezo ya Jumla:

Mungu anaenedelea kunena na Ezekieli.

Uzao wao

Uzao wa kizazi kilichopita cha Israeli aliye asi juu ya Mungu, inawarejelea watu wa wa Israeli kipindi Ezekeieli anapoandika.

sura za kikaidi na mioyo miguma

Maneno "sura za kikaidi" inarejelea jinsi walivyotenda nje, na neno "moyo mgumu" inarejea jinsi wafikiriavyo na kusikia. Yote yanasisitiza kwamba watu wa Israeli hawatabadilika jinsi walivyoishi ili kumtii Mungu.

wana nyuso za kikaidi

"wana sura kwenye nyuso zao zinazoonyesha kwamba ni wakaidi"

kaidi

"wasiotaka kubadilika"

moyo mgumu

Jiwe haliwezi kubadilika na laini, na hawa watu hawawezi kubadilika na kujuta wakati wafanyapo mambo maovu.

nyumba

Huu ni mfano kwa ajili ya familia inayoishi katika nyumba, kwa kesi hii Waisraeli, uzao wa Yakobo zaidi ya miaka mingi. "kundi la watu"

nabii alikuwa miongoni mwenu

"yule waliye mkataa kumsikiliza alikuwa nabii"

Ezekiel 2:6

Maelezo ya Jumla:

Mungu anaendelea kunena na Ezekieli

mwana wa Adamu

"Mwana wa mwanadamu" Mungu anamuita Ezekieli kusisitiza kwamba Ezekieli ni mwanadamu tu. Mungu ana nguvu na huishi milele, lakini watu hawaishi milele.

mitemba na miiba na ... nge

Haya maneno yanawaeleza wana wa Israeli ambao watamtendea Ezekieli ukarimu wakati awaambiapo ambavyo Mungu asemavyo.

mitembe na miiba

Mitembe ni vichaka vilivyochongoka juu ya matawi. Zile sehemu zilizochongoka juu ya matawi zinaitwa miiba.

nge

Nge ni mnyama mdogo mwenye kucha mbeli, miguu sita, na mkia mrefu pamoja na mwiba wenye sumu. Mwiba wake una maumivu makali sana.

Usiyaogope maneno yao

"Usiyaogope yale wasemayo."

hofu kwa nyuso zao

Neno "nyuso zao" ni mfano kwa ujumbe watu wanaueleza kwa nyuso zao. "poteza shauku kuniokoa kwa sababu ya jinsi wakutazamavyo"

Ezekiel 2:7

Maelelzo ya Jumla:

Mungu anaendelea kunena na Ezekieli.

ni waasi mno

"ni waasi sana" au "kuasi kabisa juu yangu"

nyumba

Huu ni inasimama kwa familia inayoishi katika nyumba, kwa kesi hii Waisraeli, uzao wa Yakobo zaidi ya miaka mingi.

Ezekiel 2:9

na mkono ulikuwa umenyooshwa kwangu

Ilikuwa kana kwamba, mtu katika mbingu alinyoosha mkono kumwelekea Ezekieli na Ezekieli angeweza kuona kutoka mkono hata kiwiko au bega

hati moja ya kukunja

"hati iliyokuwa imeandikwa"

Aliisambaza

Neno "Yeye" inarejelea kwa "yule aliyefanana na mtu" (1:26).

ilikuwa imeandikwa sehemu zote mbele na nyuma yake

"mtu mmoja alikuwa ameandika pande zote mbele na nyuma yake"

yaliandikwa maombelezo, huzuni na majonzi

"maombolezo," "huzuni," na "majonzi" "mtu mmoja aliandika juu yake kwamba hawa watu watahuzunika, kuhuzunika vile watakavyokuwa kama yule waliyempenda alikufa, na kuwa na mambo mabaya yaliwatokea"

Ezekiel 3

Ezekiel 3:1

Maelezo ya Jumla:

Ezekieli anaendelea kuelelza kuhusu maono aliyoyaona.

Alinambia

Neno "Yeye" inarejelea kwa ""yule aliyefanana na mwanadamu" (1:26).

Mwanadamu

"Mwana wa mwanandamu" Mungu anamuita Ezekilei hivi kusisitiza kwamba Ezekieli ni mwanadamu tu. Mungu ana nguvu na huishi milele, lakini watu hawataishi milele.

umepata nini

Hii inarejelea kwa hati ya kukunja ambao Mungu aliyokuwa akimpa.

nyumba ya Israeli

Neno "nyumba" ni mfano kwa familia inayoishi katika nyumba, katika kesi hii Waisraeli, uzao wa Yakobo zaidi ya miaka mingi. "kundi la watu wa Israeli"

hiyo hati ya kukunja

Matoleo mengi yana "hati ya kukunjua" au "hii hati ya kukunjua."

lisha tumbo lako na jaza tumbo lako kwa hii hati ya kukunjua

Neno "tumbo" linarejelea kwenye sehemu ya mwili watu wanayoweza kuiona kutoka nje. Neno "tumbo" linarejelea ndani ya ogani ndani ya tumbo.

ilikuwa tamu kama asali

Asali ina ladha tamu, na hati ya kukunjua inaladha tamu.

Ezekiel 3:4

Maelezo ya Jumla:

Ezekieli anaendelea kutueleza kuhusu maono aliyoyaona.

akanambia

"yule aliyefanana na mwanadamu" (1:26). Hakuwa "roho."

nyumba ya Israeli

Neno "nyumba" ni mfani kwa familia inayoishi katika nyumba, katika kesi hii Waisraeli, uzao wa Yakobo zaidi ya mika mingi. "kundi la Waisraeli"

maneno ya kushangaza au lugha ngumu

"anayenena manenu magumu"

sio kwa taifa lenye nguvu la maneno magumu

"Sikupeleki kwa taifa lenye nguvu ambalo watu wananena maneno magumu"

Kama nikikupeleka kwao, wataweza kukusikiliza

Hii ni hali swali lisilohitaji kujibiwa ambalo litatokea lakini halitatokea. Yahwe hakumsimamisha Ezekieli kwa watu ambao hawakuweza kuelewa lugha yake.

Kama nikikupeleka

Neno "wao" linarejelea kwa taifa lenye nguvu tofauti na Israeli.

paji gumu na moyo mgumu

"uasi sana" au "kaidi sana"

paji gumu

lisilotaka kubadilika

moyo mgumu

Hili neno linashauri kwamba watu humpinga Mungu na hawataki kumtii. Moyo umetumika kueleza sehemu katika mwili ambapo mtu huamua kile wanachotaka kukifanya.

Ezekiel 3:8

Maelezo ya Jumla:

Roho wa Mungu anaendelea kunena na Ezekieli.

Tazama!

Neno "Tazama" hapa linamtaharisha Ezekieli kuwa makini kwa habari mpya inayofuata.

Nimeufanya uso wako wa ukaidi kama nyuso zao

Neno "sura" limetumika kusimama kwa ajili ya watu. "Nimekufanya kaidi kama walivyo."

Nimekufanya ... paji la uso kuwa gumu kama mapaji yao

"Paji" ni sehemu ya mbele ya kichwa au nyusi za macho na ni mfano wa mtu. "Nimefanya ... wewe imara ili usisimame kufanya unachokifanya"

nimezifanya nyusi zako kama almasi, ngumu kama jiwe la kiberiti

"Nimezifanya nyusi zako kama jiwe gumu kabisa, nguma kuliko jiwe gumu sana."

jiwe gumu sana

jiwe ambalo ni gumu kuanzisha moto kwa kulichoma kwa chuma au jiwe jingine

nyumba

Huu ni mfano wa familia inayoishi katika familia, kwa kwesi hiiWaisraeli, uzao wa Yakobo zaidi ya miaka mingi. "kundi la watu"

Ezekiel 3:10

wachukulie kwenye moyo wako na wasikilize kwa masikio yako

"wakumbuke na wasikilize kwa makini"

Kisha nenda kwa mateka

Neno "mateka" inarejelea kwa watu wa Israeli waliokuwa wakiishi katika Babebli.

watu wako

"kundi la watu wako." Ezekieli aliishi katika Yuda kabla Wababeli kumchukua kwenda Babeli.

Bwana Yahwe

Hili ni jina la Mungu.

Ezekiel 3:12

Maelezo ya Jumla:

Ezekieli anaendelia kueleza kuhusu maono aliyaona.

nikasikia nyuma yangu sauti yenye tetemeko la aridhi: "Ubarikiwe utukufu wa Yahwe kutoka mahali pake!"

Baadhi ya matoleo yanachukua "Baraka .. mahali!" kama maneno ambayo "tetemeko kubwa" iliyonenwa. "Nimesikia nyumba yangu sauti ya tetemeko kubwa, lisemalo, 'Utukufu u kwa Yahwe kutoka mahali pake!"'

sauti ya tetemeko kubwa

Haiko wazi kama sauti ilitoka kutoka kwenye tetemeko, kutoka kwenye sauti kulikuwa na sauti kubwa kama tetemeko, au kutoka kwenye mabawa na magurudumu. sauti kama sauti ya tetemeko kubwa" au "sauti ikinena; sauti ilisikika kama tetemeko kubwa"

utukufu wa yahwe

sifa kuu ya Yahwe

sauti ya tetemeko kuu

"sauti kuu na ngurumo yenye nguvu kama sauti ya tetemeko"

Ezekiel 3:14

Maelezo ya Jumla:

Ezekieli anaonekana alinkuwa na hasira kwa sababu Yahwe alimpeleka kunena na watumwa Waisraeli, hivyo kuasi juu ya Yayhwe mwenyewe. Ingawa alipaswa kunena nao, alikuwa kimya kwa mda wa siku saba, ingawa aliisikia hasira ya Yhawe.

kwa uchungu katika hasira kali rohoni mwangu

Neno "uchungu" na "hasira" ni aina ya hasira. "nilikuwa mwenye uchungu na roho yangu alikuwa amejaa hasira" au "nilikuwa na uchungu sana na hasira."

uchungu

Ezekieli anazungumzia hasira yake kwa Yahwe kana kwamba kulikuwa na ladha mbaya kinywani kwa sababu Yahwe alimlazimisha kitu ambacho kinaladha mbay.

kwa kuwa mkono wa Yahwe alikuwa na nguvu zikigandamiza juu yangu

Ezekieli anazungumzia kuwa na huzuni na kuchoka kwa sababu Yahwe alimwamuru kufanya mambo ambayo hakuyataka kuyafanya kana kwamba Yahwe alikuwa akimsukuma chini kwenye nchi.

mkono wa Yahwe

neno "mkono" mara nyingi limetumika kurejea nguvu ya mtu au tendo "uweza wa Yahwe."

Tel Abibu

Mji katika Babeli, kama kilomita 80 kusini mashariki mwa mji mkuu, ambayo iliitwa Babeli pia.

Kebari Kanali

Huu mtu ambao watu katika Kaldea walichimba kupeleka maji kwenye bustani zao.

kushinda katika mshangao

"kutoweza kufanya jambo lolote kwa sababu nilikuwa nimeshangazwa"

Ezekiel 3:16

Maelezo ya Jumla:

Ezekieli anaeleza kuhusu uzoefu wake huko Tel-Abibu.

neno la Yahwe likanijia

"Yahwe alinena nami."

mwangalizi

Mungu alimwambia Ezekieli kuwaonya wana wa Israeli kama mwangalizi alivyowaonya watu wa mji kama maaduli walikuwa wakija, hivyo wangeweza kujiandaa na kuwa salama.

nyumba ya Israeli

Neno "nyumba" inasimama kwa ajili ya familia iishiyo katika nyumba, kwa kesi hii Waisraeli, uzao wa Yakobo zaidi ya miaka mingi. "kundi la watu Waisraeli"

onyo kwa waovu kuhusu matendo yao maovu ili aishi

"onyo kwa watu waovu kuacha kufanya mambo yake maovu ili aweze kuishi"

mwovu

"watu waovu"

kutaka damu yake kutoka kwenye mkono wako

Hii ni lugha inayoshikilia wajibu au hatia ya kuua. "nitakutenda kana kwamba ulikuwa umemuua"

hawezi kugeuka kutoka uovu wake au kutoka matendo yao maovu

Neno "matendo maovu" maana yake kitu kimoja kama "uovu." hakuacha kufanya mambo maovu."

Ezekiel 3:20

weka kizuizi mbele yake

"fanya jambo baya litokee kwake" au "kumfanya atende dhambi wazi."

atakufa katika dhambi yake

"atakufa mapema" au "atakufa kama mtu mwenye hatia kwa sababu hajanitii"

nitaiaka damu yake kutoka mkono wako

Hii ni lugha ya kushikilia wajibu wa mtu au hatia ya uuaji. "nitakutenda kana kwamba ulikuwa umemuua"

kwa kuwa alikuwa ameonywa

"tangu ulipomuonya"

Ezekiel 3:22

mkono wa Yahwe

Neno "mkono" mara nyingi limetumika kurejea kwa nguvu ya mtu au tendo. "nguvu ya Yahwe."

utukufu wa Yahwe

fahari ya Yahwe

Kebari Kanali

Huu ni mto ambao watu katika Kaldea waliuchimba kupatia bustani zao maji.

nikaanguka kifudifudi

"nikasujudu chini hata chini" au "nikalala kwenye nchi." Ezekieli hakuanguka kwa ajali. Alianguka chini hata chini kuonyesha kwamba aliheshimu na kumuogopa Yahwe.

Ezekiel 3:24

akanena nami

"yule aliyefanana na mtu." Hakuwa "Roho."

wataweka kamba juu yako na kukufunga ili usiweze kutoka nje miongoni mwao

Hii ni tafsiri nzuri halisi.

Ezekiel 3:26

Maelezo ya Jumla:

Roho anaendelea kunena na Ezekieli.

paa ya kinywa chako

"juu ya kinywa chako"

utakuwa kimya

"hutaweza kunena"

nyumba

Hii ni mfano kwa ajili ya familia iishiyo katika nyumba, katika kesi hii Waisraeli, uzao wa Yakobo zaindi ya mika mingi. kundi la watu"

nitakufungua kinywa chako

"nitakufanya uweze kunena"

yule atakayeshindwa kusikiliza hataweza kusikiliza

"yule akataaye kisikiliza hataweza kusikiliza"

Bwana Yahwe

Jina la Mungu

Ezekiel 4

Ezekiel 4:1

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na Ezekieli. Anamwambia Ezekieli kuchukua tofali na udongo na vipande vya mbao na kutenda kana kwamba alikuwa Yahwe akiuharibu mji wa Yerusalemu.

mwanadamu

"mwana wa mwanadamu" Mungu anamwita Ezekieli hivi kusisitiza kwamba Ezekieli ni mwanadamu tu. Mungu ananguvu na anaishi milele, lakini watu hawaishi milele.

chonga mji wa Yerusalemu

"chonga picha ya mji wa Yerusalemu"

laza ngome juu yake

"zunguka mji ili kuunyakua"

jenga ngome juu yake

"jenga kuta juu yake." "Kuta zitawahifadhi watu wasiuache mji.

Anza kushambulia juu yake

"jenga hanamu nje ya hiyo kwa ajili ya maadui kuingia ndani." Yerusalemu ilikuwa na ukuta kuizunguka kuwalinda watu ndani.

Weka shambulio la ghasia kuizunguka

"Shambulio la ghasia" ni miti mikubwa au nguzo ambazo watu katika vita wangechukua na kupiga juu ya ukuta au mlango hivyo wangeuangusha chini na kuingia ndani. "Weka kuizunguka nguzo kubwa watu watumie kuvunja malango na kuingia ndani"

weka uso wako juu yake

"itazame kwa uso wa hasira"

nyumba ya Israeli

Neno "nyumba" ni mfano wa familia iishiyo katika nyumba, katika kesi hii Waisraeli, uzao wa yakobo zaidi ya miaka mingi.

Ezekiel 4:4

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anendela kunena na Ezekieli.

weka dhambi ya nyumba ya Israeli juu yake

"teseka kwa kulaza upande wako kwa sababu ya dhambi zao."

nyumba ya Israeli

Neno "nyumba" ni mfano wa familia iishiyo katika nyumba, kwa kesi hii Waisraeli, uzao wa Yakobo zaidi ya miaka mingi iliyopita.

utachukua dhambi zao

"utakuwa na hatia za dhambi zao" au "utaadhibiwa kwa ajili ya dhambi zao"

lala chini juu ya nyumba ya Israeli

"lala kuelekea ufalme wa Israeli."

Mimi mwenyewe nakuagiza kwako siku moja kuwakilisha kila mwaka wa adhabu yao

"Mimi mwenyewe nimekuamuru kulala upande wako kwa namba ile ile ya siku kama namba ya miaka ambayo nitakayo waadhibu."

kila mwaka wa ghadhabu yao

kila mwaka watakaoadhibiwa kwa ajili ya dhambi zao

Ezekiel 4:6

Maelezo ya Jumla:

Roho anaendelea kunena na Ezekieli.

siku hizi

siku Ezekieli alipolala chini upande wake wa kushoto kuelezea ngome ya ufalme wa Israeli

utachukua uovu

"utakuwa na hatia ya uovu" au "utaadhibiwa kwa ajili ya uovu wao."

Nyumba ya Yuda

Neno "nyumba" ni mfano wa familia iishiyo katika nyumba, katika kesi hii uzao wa Yuda zaidi ya miaka mingi. "kundi la watu wa Yuda" au "watu wa Yuda"

Nakuteua siku moja kwa kila mwaka

"Nitakufanya kufanya kufanya siku moja kwa kila mwaka ambao nitakughadhibu."

tabiri juu yake

"tabiri kuhusu mambo mabaya yatakayotokea kwa Yerusalemu"

tazama!

"ona!" au "sikiliza!" "kuwa makini kwa kile ninachotaka kukwambia!"

Naweka vifungu juu yako

Vifungo ni kamba au minyororo inayomfanye mtu asitembee. Haiko wazi kama neno "vifungo" ni mfano kwa jambo Yahwe analolifanya ambalo ni kama alikuwa amemfunga Ezekieli

Ezekiel 4:9

Maelezo ya Jumla:

Roho anaendelea kunena na Ezekieli.

ngano, shayiri, ... mtama, na kusemethi

Hii ni aina tofauti tofauti za nafaka.

maharagwe

mbegu za mizabibu, ambao humea katika safu moja ndani yake njia nyingine tunda tupu, linaweza kuliwa

dengu

Haya ni kama maharagwe, lakini mbegu zake ni ndogo, mviringo, na sawasawa.

shekeli ishirini kwa siku

"shekeli 20 kwa siku." gram 200 za mkate kila siku"

sita ya hini

" hini1/6" au "sehemu ya sita ya hini" au "takriban nusu lita" (UDB)

Ezekiel 4:12

Maelezo ya Jumla:

Roho anaendelea kunena na Ezekieli.

Utalila

mkate

shayiri

mkate bapa wa shayiri

keki za shayiri

mkate wa bapa uliotengenezwa na shayiri

utauoka kwenye kinyesi kikavu cha mwanadamu

"utaupika juu ya moto uliotengenezwa kwa viapande vya uchafu mgumu wa mwanadamu."

nitawafukuza

peleka mabali kwa nguvu

Ezekiel 4:14

Ee

Ezekieli anataabika kwa kile Bwana alichomwambia afanye. "Itakuwa si sawa kwa mimi kufanya hivyo"

Bwana Yahwe

Jina la Mungu. Hapa Ezekieli ananena na Bwana.

nyama ya kunuka

Hii inarejea kwa nyama ambayo ni najisi kwa sababu imekuja kutoka mnyama aliyekufa kwa ugonjwa au aliyezeeka au aliyeuawa na mnyama mwingine. Neno "kunuka" hunyesha karaha yake juu ya nyama kama hii. "kuchukiza, nyama najisi"

nyama ya kunuka haijawahi kuingia katika kinywa changu

"sijawahi kula nyama ya kunuka."

Tazama!

"Sikia" au "kuwa makini kwa jambo la muhimu nitakalokwambia sasa"

nimekupatia

"nitakuruhusu kutumia"

mbolea ya ng'ombe

uchafu mgumu kutoka kwenye ng'ombe au mbolea ya ng'ombe.

kinyama cha binadamu

uchafu wa mwanadamu.

Ezekiel 4:16

Tazama!

"Tazama!" au "Sikia!" au "Kuwa makini kwa kile ninachotaka kukwambai!"

Nalivunja gongo la mkate katika Yerusalemu

"nitasimamisha usambazaji wa chakula kwa Yerusalemu."

mkate wa gongo

Kusambaza kunaitwa gongo kwa sababu baadhi ya watu wanahitaji gongo kutembelea na kufanya kazi zao, na watu wanahitaji mkate kuishi. Mkate unawakilisha aina zote za mkate. "kusambaza chakula"

Yerusalemu

"watapungukiwa makate na maji" hata "Nalivunja gongo la mkate" ni "Yerusalemu - wata ... tetemeka - ili"

watakula mkate ukiwa unagawa katika wasiwasi

"watagawanya kwa makini mkate wao kwa sababu wanahofia kwamba hautatosha"

kugawa

kutoa kiasi kidogo cha kitu kwa watu wengi ambachi hatoshi

kugawa kwa kutetemeka

"kuugawa ukiwa unatetemeka" au "kuugawa katika hofu"

kila mtu atafadhaishwa na ndugu yake na kumpoteza

"kila mmoja atamtazama ndugu yake na kuhofu kuhusu ni kiasi gani cha chakula ndugu yake hula na kupoteza"

poteza

Hili neno mara zote limetumika nyama au kuchimbua mabao. Hapa ni mfano kwa watu waovu kuwa wembamba na kufa kwa sababu hawana chakula.

Ezekiel 5

Ezekiel 5:1

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na Ezekieli. Kila mifano ya "miji" inarejea kwa "mji" ambao Ezekieli kuchonga kwenye tofali (4:1).

mwana wa adamu

"mwana wa mwanadamu" au "mwana wa binadamu." Mungu anamwita Ezekieli hivi kusisitiza kwamba Ezekieli ni mwanadamu tu. Mungu ananguvu na huishi milele, lakini watu hawawezi kushi milele.

kiwembe cha kinyozi

"ubapa kwa ajili ya kunyolea nywele"

pitisha wembe juu ya kichwa chako na ndevu

"nyoa kichwa chako na uso wako" au "ondoa nywele zako kutoka kichwa chako na ndevu kutoka uso wako"

Choma theluthi ya tatu ya hiyo

"Choma theluthi ya tatu ya nywele zako"

kati

katikati

wakati siku za ngome zitakapokamilika

"wakati siku za ngome ya Yerusalemu zitakapoisha"

chukua theluthi ya tatu ya nywele

"chukua moja ya tatu ya manyoya ya nywele"

na uipige kwa upanga kuzunguka mji wote

"na ipige kwa upanga wako mji wote"

tawanya theluthi yake kwenye upepo

"ruhusu upepo uvume theluthi ya mwisho ya nywele zako katika mwelekeo tofauti"

Nitasogeza upanga kufata watu

Neno "upanga" ni mfano kwa ajili ya adui maaskari ambao watawashambulia kwa panga zao, na kwa "kusogeza upanga" ni kupeleka maadui kuwafatilia na kuwashambulia kwa uapanga. (UDB)

Nitakusogoza mbali kwa upanga

"Nitauvuta upanga nje ya kibebeo chake"

Ezekiel 5:3

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na Ezekieli.

Lakini chukua ... kisha chukua

Ezekieli alikuwa afanye hivi wakati aliponyoa nywele zake na ndevu (5:1) na kabla hajachoma nywele (5:1).

hesabu ndogo ya nywele kutoka kwao

"nywele chache kutoka manyoya laini ya nguo"

zifunge

Neno "wao" inarejelea nywele. nywele zilkuwa ndefu tayari hivyo Ezekieli angeweza kuzifunga.

pindo za nguo zako

Maana ziwezekanazo 1) "nguo kwenye mikono yako" ("mikono ya vazi lako") (UDB) au 2) mwishoni mwa vazi kwenye joho lako" (pindo lako").

kutoka hapo utatoka nje kwenda nyumba zote za Israeli

"kutoka huko moto utasambaa na kuwachoma watu wote wa Israeli." Yahwe anazungumzia jinsi atakavyo iadhibu Israeli kana kwamba alikuwa akienda kuweka moto kwenye nyumba na watu wa Israeli kana kwamba walikuwa familia iishiyo katika nyumba.

nyumba ya Israeli

Neno "nyumba" mfano kwa ajili ya familia iishiyo katika nyumba, katika kesi hii Waisraeli, uzao wa Yakobo zaidi ya miaka mingi. "kundi la watu wa Israeli"

Ezekiel 5:5

Maelezo ya Jumla:

YAhwe anaendelea kunena.

Bwana Yahwe

Jina la Mungu

Hii ndio Yerusalemu

"Hili pango linawakilisha Yerusalemu"

katikati ya Mataifa

Maana ziwezekanazo 1) mataifa mengine yalikuwa pande zote za Yerusalemu au 2) "muhimuz aidi kuliko mataifa mengine."

nimemuweka

Yerusalemu inarejelewa kama "yeye" na "-kike."

nchi nyingine

"nchi jirani" au "nchi zinazozunguka"

Watu wamezikataa hukumu zangu

"Watu wa Israeli na Yerusalemu wamekataa kutii hukumu zangu."

Ezekiel 5:7

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na watu wa Israeli na Yuda.

Bwana Yahwe

Jina la Mungu

Kwa sababu mmekuwa kikwazo kuliko

"kwa sababu hali yenu ya dhambi ni mbaya kuliko" au "kwa sababu ninyi ni makaidi kuliko"

yanayowazunguka

"yote yanayowazunguka."

kuacha kuenenda katika amri zangu

"Kuenenda ni mfano kwa njia mtu aishiyo. "kutokuishi kulingana na amri zangu" au "bila kuzitii amri zangu"

au tenda kulingana na maagizo yangu

"au kutii maagizo yangu"

Tazama!

"Tazama!" au "Sikia" au "Kuwa maini kwa kile nnachotaka kukwambia!"

nitatekeleza hukumu kati yako

"nitakuhumu katika njia tofauti tofauti" au "nitakuadhibu" (UDB).

Ezekiel 5:9

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na watu wa Israeli na Yerusalemu.

yale ambayo sijawahi kuyafanya na kile ambacho sintokifanya tena

"kama sijawahi kufanya na sintafanya katika njia ile ile tena" au "kama sijawahi kufanya tena na sitafanya tena" (UDB).

Kwa sababu ya matendo yenu maovu

"kwa sababu ya matendo yenu yote maovu muyafanyayo." Mungu alikuwa na hasira kwa sababu watu walikuwa wakiabudu sanamu na miungu ya uongo.

mababa watawala watoto wao kati yenu, na wana watawala baba zao

Huenda Ezekieli anaeleza nini kitatokea hasa wakati watakapo kosa chakula.

nitatekeleza hukumu juu yako

"nitakuhukumu" au "nitakuadhibu kwa ukali" (UDB)

na kuwatawanya kila upande wote walio ondoka

"na nitawalazimisha wote walio ondoka kwenda sehemu tofauti tofauti."

Ezekiel 5:11

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na watu wa Israeli na Yuda.

ishi-huu ndio usemi wa Bwana Yahwe-hii

Yahwe anajinenea yeye mwenyewe kana kwamba kulikuwa na mtu mwingine, au Ezekieli anawakumbusha wasomaji wake kwamba anamnukuu Yahwe.

kama niishivyo

"kama niishivyo hakika." au "kama kweli iko hivyo ni hai, ni hakika pia kwamba"

Bwana Yahwe

jina la Mungu

najisi ... patakatifu

haribu mahali ambapo Yahwe alipokuwa ameweka karibu kuwa kwa matumizi yake pekee

kwa mambo ya yanayoumiza

"kwa mambo yote yako yanayoumiza." "kwa sanamu zako zote, nizichukiazo" au "kwa sanamu zako zote za kuchukiza" (UDB)

na kwa matendo yako maovu

"na kwa mambo yenu yote ya machkizo mliyoyafanya"

jicho langu halitakuwa na huruma juu yako

Neno "jicho" ni mfano wa Yahwe. "sitakuwa na huruma juu yako"

sitokuharibu

"nitakuadhibu hakika"

wataliwa kwa njaa kati yako

"wengi wao watakufa kwa sababu ya njaa"

Ezekiel 5:13

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na watu wa Israeli na Yuda.

ghadhabu yangu itatimia

"sitakuwa na hasira tena kwa sababu nimefanya kila kitu nilichotaka kukifanya kwa sababu nilikuwa na njaa"

nitaifanya ghadhabu yangu juu yao hata kulala

Neno "ghadhabu" maana yake hasira kali sana, na hapa inarejelea kwa adhabu. "nitaacha kukuadhibu kwa sababu nimewaadhibu kwa uaminifu."

nitaridhika

"nitaridhika kwamba nimewaadhibu mno"

wakati nitakapokamilisha ghadhabu yangu juu yao

"wakati nitakapomaliza kuwaadhibu"

Ezekiel 5:15

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na watu wa Israeli na Yuda.

katika hasira na ghadhabu

Neno "hasira" na "ghadhabu" kimsingi yana maana moja na kusisitiza mkazo wa hasira. "kwa sababu nitakuwa na hasira nanyi mno."

mishale mikali

"mkazo wa njaa"

vunja gongo lenu la mkate

"Gongo" kilikuwa kitu ambacho watu waliegama juu ya kuwasaidia. Hili neno ni mfano maana yake "kuondoa kusambaza chakula ambacho ukitegemeach." "katilia chakula chenu" (UDB)

Pigo na damu vitapita juu yenu

"Pigo na kifo kikali sana kitapita juu yenu." Hiki kifo kikali kitasababishwa na vita.

Ezekiel 6

Ezekiel 6:1

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anamwambia Ezekieli kunena na milima kana kwamba walikuwa watu ili kwamba watu wa Israeli wangesikia maneno na kujua kwamba maneno ya Ezekieli yalikuwa kwa ajili yao.

Neno la Yahwe likanijia

"Yahwe akanena nami."

Mwana wa adamu

"Mwana wa mwanadamu" au "Mwana wa bianadamu."

weka uso wako juu ya milima ya Israeli

"tazama milima ya Israeli kwa uso wa nguvu."

milima ya Israeli

"milima ya Israeli katika nchi ya Israeli."

Tazama!

"Tazama!" au "Sikiliza!" au "Kuwa makini kwa kile ninachotaka kukwambia!"

Bwana Yahwe

Jina la Mungu

naleta upanga juu yako

Neno "upanga" hapa linarejelea vita. "ninaleta vita juu yako."

Ezekiel 6:4

Maelezo ya Jumla:

Haya ni maneno ya Yahwe kwa watu wa Israeli.

Kisha madhabahu zenu zitakuwa ukiwa na nguzo zenu zitaharibiwa

"Hakutakuwa na yeyote wakuabudu madhabahu zenu na adui wataziharibu nguzo zenu"

nitwatupa chini ... nitailaza ... na kutawanya

Yahwe alikuwa akinena juu ya kuwapeleka maaskari kuwatupa chini ... watalala ... na kutawanya."

maiti zenu

"watu wenu waliokufa"

Ezekiel 6:6

Maelezo ya Jumla:

Haya ni maneno ya Yahwe kwa watu wa Israeli.

miji itaharibiwa

"Wanajeshi maadui wataiharibu miji yenu"

zitavunjwa

"madhabahu zenu zitavunjwa" au "wanajeshi maadui watazivunja."

nguzo zenu zitaangushwa chini

"wataziangusha nguzo zenu."

kazi zenu zitafutiliwa mbali

"hakuna atakayekumbuka ulichokifanya"

Maiti zitaanguka chini kati yenu

"Umuona adui akiwaua watu waengi"

jua kwamba mimi ndiye Yahwe

Maana ziwezekanazo ni 1) "tambua mimi, Yahwe, ni nani" au 2) "tambua kwamba mimi ni Yahwe, Mungu wa kweli."

Ezekiel 6:8

Maelezo ya Jumla:

Haya ni maneno ya Yahwe kwa watu wa Israeli.

baadhi yao ambao walioukimbia upanga

"baadhi yao waliouawa katika vita." Upanga unawakilisha kuuawa katika vita.

wakati mtakapo tawanyika miongoni mwa nchi tofauti tofauti

"wakati mtakapoenda ishi katika nchi tofauti tofauti"

nitakavoyowaponda mioyo yao ya kikahaba ambayo imeniacha

Yahwe anawazungumzia Waisraeli kana kwamba walikuwa mwanamke anayelala na watu wengi. "nilikuwa na huzuni kwa sababu walikuwa kama mke aliyeniacha na kulala na wanaume wengine"

na kwa macho yao ya kikahaba kufuata sanamu zao

Yahwe anawazungumzia Waisraeli kana kwamba walimuoa mwanamke anayetafuta wanaume wengine na kutamani kulala nao. "na kwa njia waliyoitamani kwa nguvu kuabudu sanamu"

wataonyesha chuki kwenye nyuso zao kwa udhaifu walioufanya

Maana zinazowezekana ni 1) "watajichukia wenyewe kwa sababu ya mambo yao maovu waliyoyafanya" au 2) "watayachukia mambo maovu waliyoyafanya." "Nyuso zao zitaonyesha chuki zao kwa uovu walioufanya."

Ezekiel 6:11

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na Ezekieli.

Bwana Yahwe

Jina halisi la Mungu wa Kweli alilojifunua kwa wa Israeli.

Piga makofi na kanyaga kwa mguu wako

Ezekieli alikuwa afanye hili tendo la ishara kupata umakini wa watu. Hii haikuwa makofi.

Ole

Neno "Ole" limetumika kuelezea huzuni.

nyumba ya Israeli

Neno "nyumba" ni mfano kwa ajili ya familia iishiyo katika nyumba, katika kesi hii Waisraeli, uzao wa Yakobo zaidi ya miaka mingi. "kundi la watu wa Israeli"

Kwa kuwa wataanguka kwa upanga, njaa, na tauni.

"Kwa kuwa watakufa kwa upanga, njaa, na tauni." "Upanga", "njaa", na "tauni" ni njia mbali mbali watakazokufa. Upanga "upanga" inawakilisha vita.

nitaikamilisha ghadhabu yangu juu yao

"nitatosheleza hasira yangu juu yao"

Ezekiel 6:13

Maelezo ya Jumla:

Haya ni maneno ya Yahwe kwa watu wa Israeli.

jua kwamba mimi ndimi Yahwe

Maana zinazowezekana ni 1) "tambua mimi ndiye, ambaye, Yahwe, au 2)"tambua kwamba mimi Yahwe, ndiye Mungu wa kweli"

kuzunguka madhabahu zao, kwa kila mlima mrefu

Maana nyingine inayowezekana ni "kuzunguka madhabahu zao, ambazo zipo katika kila mlima mrefu"

mlima mrefu-juu ya vilele vya mlima, na chini ya mti wenye majani mabichi na mwaloni

Maana nyingine zinazowezekana ni "mlima, juu ya vilele vya milima yote, chini ya mti uliostawi, na chini ya kila mwalo mkubwa."

kustawi

yenye afya na inayokua

mwaloni

mti mkubwa wenye mbao imara zinazo andaliwa kwa ajili ya kivuli cha kuabudia

Dibla

Baadhi ya maandiko yanasema Ribla. Hili lilikuwa jina la mji katika kaskazini.

Ezekiel 7

Ezekiel 7:1

Maelezo ya Jumla:

Hii inaanza na utabiri wa hukumu ya Yahwe juu ya Israeli.

Neno la Yahwe likanijia

"Yahwe akanena nami."

Wewe, mwana wa adamu

"Mwana wa adamu, nataka uwe makini kwa kile ninachoenda kukwambia"

Bwana Yahwe

Hili jina la Mungu wa kweli alilojifunua katika taifa la Israeli.

kwa nchi ya Israeli

"kwa watu wa Israeli".

Mwisho!

"Mwisho umefika!"

mipaka minne ya nchi

Hii inarejelea kwa nchi nzima ya Israeli.

Ezekiel 7:3

Maelezo ya Jumala:

Haya ni maneno ya Yahwe kwa watu wa Israeli

mwisho uko juu yako

"uhai wako umeisha" au "mwisho wa mda wako umefika"

kutokana na njia zako

"kulingana na mambo unayoyafanya" au "kwa sababu ya mambo maovu ufanyayo"

nitaleta machukizo yako yote juu yako

"nitaufanya uzoefu wako matokeo ya tabia yako ya machikizo" au "nitakuadhibu kwa kufanya haya mambo ninayoyachukia sana"

machukizo

Hii inarejelea kwa tabia ambayo Mungu aichukiayo.

Kwa kuwa macho yangu hayatakuhurumia

"Kwa kuwa sitakutazama kwa huruma"

nitaleta njia zako juu yako

"nitakufanya mzoefu wa matokeo ya tabia yako mbaya" au "nitakuadhibu kwa mambo mabaya uyafanyayo."

machukizo yako yatakuwa katikati yako

"matokeo ya tabia yako ya chuki yatakuzunguka" au 2) "sanamu zako zitakuwa pamoja nawe na hazitakuwa na uwezo."

Ezekiel 7:5

Maelezo ya Jumla:

Haya ni maneno ya Yahwe kwa watu wa Israeli.

Bwana Yahwe

Jina la Mungu linaloonyesha kwamba yeye ni Mungu wa uwezo wote.

Msiba! Msiba wa pekee! Tazama, unakuja.

Hili tamko linamaanisha kufanya ujumbe imara sana. "Tazama, msiba wa kutisha unakuja, ambao hakuna ambaye amewahi kuupata."

Tazama

Neno "tazama" hapa linaongeza msisitizo kwa kile kifuatacho. "Tazama" au "Sikiliza" au "Kuwa makini kuhusu ninachotaka kukwambia."

Mwisho umeinuka juu yako

Hukumu inayokuja inachukuliwa kana kwamba alikuwa adui akiamka kutoka usingizini.

milima haitakuwa na shangwe tena

"watu juu ya milima hawatakuwa na shangwe tena."

Ezekiel 7:8

Maelezo ya Jumla:

Haya ni maneno ya Yayhwe kwa watu wa Israeli.

Sasa hivi punde

"Hivi punde baada ya mda mfupi sana"

nitamwaga ghadhabu yangu juu yako na kujaza hasira yangu juu yako

Yahwe anatumia haya maneno "mwaga" na "kujaza" kulinganisha utendaji wake na kumwaga maji na kujaza chupa. Haya maneno mawili kimsingi yana maanisha kitu kimoja na kusisitiza ukali wa adhabu ya Yahwe. "nitakiuadhibu vikali kwa sababu ninahasira sana.."

ghadhabu

"hasira" au "hasira kubwa"

Kwa kuwa jicho langu halitatazama kwa huruma

Neno "jicho langu" linamaanisha Mungu mwenyewe. "Kwa kuwa sitatazama kwa huruma"

sitakuharibu

"sitakuacha bila adhabu" au "nitakuadhibu"

machukizo yako yatakuwa katikati yako hivyo utajua kwamba ni mimi Yahwe

"nitaufanya uzoefu wako matokeo ya tabia yako ya machikizo" au "nitakuadhibu kwa kufanya haya mambo ninayoyachukia sana"

Ezekiel 7:10

Maelezo ya Jumla:

Haya ni maneno ya Yahwe kuhusu Israeli.

Tazama!

"Tazama!" ai "Sikiliza" au "Kuwa makini kwa kile ninachotaka kukwambai!"

Siku inakuja

"Siku ya hukumu yako inakuja."

Kifo kimetoweka

Hii inaonyesha kwamba yamkini hicho kifo kitakuja kwa Israeli. "Kifo kimeanza kuja kwa Israeli" au "Mambo ya kuogofya yameanza kutokea."

Gongo limechipua kwa maua mengi ya kiburi

"Ua limeanza kukua juu ya fimbo na umekua pamoja na kiburi." Hapa neno gongo linawakilisha pengine Israeli au udhalimu. Maana zinazowezekana 1) "Watu wa Israeli wamekuwa na kuburi sana" au "Watu wa Israeli wamekuwa na wadhalimu na kiburi sana."

Udhalimu umekuwa kwenye gongo la uovu

"Udhalimu wa watu umewapeleka kufanya mambo maovu zaidi"

Ezekiel 7:12

Maelezo ya Jumla:

Haya ni maneno ya Yahwe kuhusu Israeli.

Wakati unakuja; siku imekaribia

Yote "mda" na "siku" zinarejelea kwenye muda wakati Mungu atakapo waadhibu watu wa Israeli. "adhabu ya Israeli itakuwa hivi punde sana"

maono yako juu yako kikundi kizima

"kile Mungu alichoonyesha kitatokea kwenye kundi"

kundi

kundi la watu wengi sana. Hapa inarelea kwa watu wa Israeli.

kadiri wanapoendelea kuishi

Neno "wao" linarejelea kwa watu wa Israeli wauzao vitu.

Hatarudi

"hawatarudi Israeli."

hakuna mtu anayeishi kwenye dhambi atakayejitia uwezo

Neno "uwezo" linamrejea msaada wa Mungu anamsaidia mtu kuendelea kwenda wakati mambo ni magumu kupitia tumaini, faraja na nguvu ya mwili. "hakuna aliye hai anayeendelea kumuasi Mungu atakayesaidiwa na Mungu."

Ezekiel 7:14

Maelezo ya Jumla:

Haya ni maneno ya Yahwe kuhusu Israeli.

Wamepiga tarumbeta

"Wamepiga tarumbeta kuwaita watu kupigana juu ya adui.

Upanga uko nje

Upaga unawakilisha mapambano au vita. "Kuna mapigano nje."

pigo la njaa lipo ndani ya jengo

Kimsing jungo hurejea kwenye mji

wakati njaa na tauni zitakapowala wale waliopo kwenye mji

Hapa neno "kula" linamaanisha "haribu kabisa." "na watu wengi katika mji watakufa kutokana na njaa na ugonjwa."

Kama hua wa mabondeni, wote watalia

Hua hufanya kambi chini kunusa hiyo milio kama mlio mtu afanyayo wakati akiwa katika maumivu ya kawaida au maumivu ya ndani.

Ezekiel 7:17

Maelezo ya Jumla:

Haya ni maneno ya Yahwe kuhusu Israeli.

na hofu kuu itawafunika

"watajawa na hofu" au "na watakuwa na wasi wasi sana"

katika siku ya ghadhabu ya Yahwe

"katika siku wakati Yahwe atakapotenda juu ya hasira yake" au "wakati Yahwe atakapowaadhibu"

hawatashibishwa njaa yao

"hawatakuwa na chakula cha kula"

uovu wao umekuwa kizuizi

Maana ziwezekanazo 1) "kwa sababu kumiliki dhahabu nyingi na fedha zimewapelekea kuasi" (UDB) au 2) "kwa sababu ni waovu, wanafanya dhambi hiyo inaonyesha jinsi walivyo waovu."

Ezekiel 7:20

Maelezo ya Jumla:

Haya ni maneno ya Yahwe kuhusu Israeli.

nitawapatia hivyo vitu kwenye mikono ya wageni

Neno "mkono" umetumika unarejelea mamlaka. "nitazitoa hizo sanamu kwenye mamlaka ya watu wasio wajua" au "nitazitoa hizo sanamu kwa watu wasio wajua"

mateka

viyu vilivyopotea au kuchukuliwa kwa nguvu

watawanajisi

Wageni na watu waovu watazinajisi sanamu ambazo watu wa Israeli walizo zitengeneza.

nitaurudisha uso wangu mbali

"sitakuwa makini" au "sitatazama"

mahali pangu pa siri

"mahali nipapendapo" Hii inarejelea kwa hekalu la Mungu.

Ezekiel 7:23

Maelezo ya Jumla:

Haya ni maneno ya Yahwe kwa Ezekieli kuhusu Israeli.

Tengeneza mnyororo

Minyororo hutumika kushikilia watumwa au wafungwa. Mungu anasema hivi kuonyesha watu ambao watakuwa watumwa au wafungwa.

nchi imejawa na hukumu ya damu

"kila sehemu katika nchi Mungu anawahukumu watu kwa sababu wamewaua watu wengine vikali sana."

mji umejaa udhalimu

"Udhalimu u kila mahali katika mji" au "watu wengi katika mji wanafanya mambo maovu kwa wengine"

na watamiliki nyumba zao

"waovu watazichukua nyumba za Israeli"

nitaleta mwisho kwenye fahari ya uweza

nitawafanya watu wenye nguvu katika Israeli kuacha kujiona fahari"

mahali pao patakatifu patanajisiwa!

Maadui watapanajisi mahali mnapo abudia."

mahali pao patakatifu

mahali ambapo walipoabudia sanamu.

Hofu itakuja

"Watu watakuwa na hofu"

Wataitafuta amani

"Watatumaini tumaini kwa ajili ya amani" au "Watajaribu kufanya amani pamoja na maadui zao"

Ezekiel 7:26

Maelezo ya Jumla:

Haya ni maneno ya Yahwe kuhusu Israeli.

watatafuta maono kutoka kwa nabii

"watawauliza manabii ni maono gani waliyoyaona."

sheria itawaangamiza kutoka kwa kuhani na shauri kutoka kwa wazee

"Hawa makuhani hawatafundisha sheria na wazee hawataweza kutoa ushauri mzuri." Hii ni kwa sababu Mungu hawapatia hekima.

mwan mfalme

Maanza zinazo wezekana 1) "mwana wa mfalme" (UDB) au 2) kila mwanmume wa familia ya kifalme isipokuwa mfalme.

atakata tamaa

Maana zinazo wezekana 1) "hatakuwa na tumaini" au 2) "atavaa mavazi ambayo yataonyesha anaomboleza."

mikono ya watu wa nchi itatetemeka kwa hofu

"watu wa nchi watakuwa na hodu kubwa kwamba mikono yao itatetemeka"

jua kwamba mimi ni Yahwe

"jua kwamba mimi, Yahwe, ndimi"

Ezekiel 8

Ezekiel 8:1

Maelezo ya Jumla:

Ezekieli anaeleza kuhusu ono jingine aliloliona.

Hivyo ikawa

Hili neno limetumika hapa kuonyesha mwanzo wa mwanzo wa sehemu ya hadithi.

katika mwaka wa sita

"katika mwaka wa sita wa uhamisho wa Mfalme Yehoyakini"

mwezi wa sita, katika siku ya tano ya mwezi

"siku ya sita ya mwezi." Huu ni mwezi wa sita wa kalenda ya Kiebrania. Siku ya tano inakaribia mwezi wa tisa katika kalenda za Magharibi.

mkono wa Bwana Yahwe ukanguka tena juu yangu

baaaye Ezekieli alipoona kitu kama mkono. Wengine wanaweza kuchagua kufikiria mkono sitiari kwa ajili ya uwepo wa Yahwe au uweza. (UDB)

Bwana Yahwe

Jina la Mungu aliye hai.

anguka juu

"shikilia"

mng'ao wa chuma

Wakati ikiwa yamoto sana, hung'aa kwa njano au mwanga wa chungwa.

Ezekiel 8:3

Maelezo ya Jumla:

Ezekieli anaendelea kueleza kuhusu maono kutoka kwa Mungu.

akanyoosha

Neno "yeye" huenda linarejelea kwa "picha kama mtu"

kati ya mbungu na nchi

"kati ya anga na ardhi"

katika maono kutoka kwa Mungu, akanileta hata Yerusalemu

Neno "katika maono" inamaana kwamba huu uzoefu unatokea katika mawazo ya Ezekieli. Angeendelea kubakia nyumbani kwake wakati Mungu anapomwonyesha haya mambo.

lango la ndani la kaskazini

"lango la ndani la kaskazini mwa hekalu"

sanamu ile iletayo wivu mkubwa

"sanamu yule aletaye wivu mkubwa" au "yule sanamu anayemsababisha Mungu kuwa na wivu"

ambaye mwonekano wake ulikuwa ule ule nilipoona katika uwanda

"aliyeonekana sawa kama yule niliyemuona katika uwanda"

uwanda

eneo kubwa la nchi ya tambarare ambalo lina miti michache.

Ezekiel 8:5

Maelezo ya Jumla:

"Picha kama ya mtu" (8:1) inanena na Ezekieli.

Mwanadamu

"Mwana wa mwanadamu" au "mwana wa binadamu."

inua macho yako juu

"tazma" au "geuza kichwa chako na tazama"

lango linaloelekea kwenye madhabahu

"lango kupitia watu wanaotembea hivyo wanaweza kwenda kwenye madhabahu"

unaona kile wanachokifanya?

Mungu anatumia hili swali kuvuta usikivu wa Ezekieli kwa kile watu walichokuwa wakikifanya. "nataka kufahamu kwa nini nachukia kile watu wanachokifanya hapa."

nyumba ya Israeli

Neno "nyumba" ni badala ya familia inayoishi katika nyumba, katika kesi hii Waisraeli, uzao wa Yakobo zaidi ya miaka mingi.

Ezekiel 8:7

ua

"ua wa hekalu"

Ezekiel 8:10

Tazama!

Neno "tazama" hapa linaonyesha kwamba Ezekieli alishangazwa kwa kile alichokiona.

Kulikuwa na kila umbo la vitu vikitembea

"vitu vilivyo chongwa katika ukuta wa kila aina ya wanyama watambaao na wanyama wa karaha." Neno kitu kitambaacho" linarejea wadudu na wanyama wengine wadogo.

nyumba ya Israeli

Neno "nyumba" linasimama badala ya familia inaishi katika nyumba, katika kesi hii Waisraeli, uzao wa Yakobo zaidi ya miaka mingi.

Yaazania mwana wa Shafani

hili ni jina la kiume

chetezo

sufuria ambayo watu hutumia kwa kuchomea ubani ndani wakati wakimwabudu Mungu au miungu ya uongo

Ezekiel 8:12

unaona kile ambacho wazee wa nyumba ya Israeli wanachokifanya kwenye giza

Mungu aliuliza hili swali hivyo Ezekieli angeona kile ambacho Mungu alichokuwa akimwambia kutazama.

nyumba ya Israeli

Neno "nyumba" ni mfano kwa ajili ya familia inayoishi katika nyumba, katika kesi hii Waisraeli, uzao wa Yakobo zaidi ya miaka mingi.

humba kilichojificha cha sanamu yake

"hapa chumba ambacho hakuna anayeweza kumuona akiabudu sanamu wake"

Ezekiel 8:14

lango la kuingia la nyumba ya Yahwe lililokuwa upande waa kaskazini

Hili lilikuwa lango la nje kaskazini sio kama lili la katika 8:3

tazama!

Neno "tazama" hapa linaonyesha kwamba Ezekieli alishangazwa kwa kile alichokiona.

wakimlilia Tamuzi

"kuhuzunika kwa sababu kwa sababu mungu wa uongo Tamuzi alikuwa amekufa.

Ezekiel 8:16

tazama!

Neno "tazama" hapa linaonyesha kwamba Ezekieli alishangazwa kwa kile alichokiona.

varanda yenye matao na nguzo

vinyago mbele ya lango la kuingia pamoja na safu au mihimili kwa ajili ya kusaidia

na ntuso zao kuelekea mashariki

"na walikuwa wakitazama kuelekea mashariki"

Ezekiel 8:17

Je ni kitu kidigo kwa ajili ya nyumba ya Yuda kufanya haya machukizo wanayoyafanya hapa

Mungu anatumia hili swali kuonyesha hasira yake ambayo watu wa Yuda hawafikirii kwamba kuabudu sanamu ni kitu kibaya sana.

nyumba ya Yuda

Neno "nyumba" ni mfano kwa ajili ya familia iishiyo katika nyumba, katika kesi hii uzao wa Yuda zaidi ya miaka mingi.

wameijaza nchi kwa udhalimu

"nchi yote wanafanya mambo ya udhalimu au "nchi yote wanashambuliana kila mmoja"

kunichochea hasira

"kunikasirisha"

kuweka tawi kwenye pua zao

Hii inaweza kumaanisha "kushikilia matawi kwenye pua zao katika ibaada ya uongo."

sitaacha kuwaharibu

"bado nitawaadhibu."

hata watalia kwenye masikio yangu kwa sauti kubwa

"Hata watapiga yowe kwangu kwenye maombi yao kwa sauti kubwa"

sitawasikia

"sitawasikiliza"

Ezekiel 9

Ezekiel 9:1

Maelezo ya Jumla:

Ezekieli anaendelea kueleza kuhusu maono aliyopewa na Mungu.

akalia katika masikio yangu

"nilimsikia akiniita kwa sauti"

walinzi

watu ambao hulinda kitu.

silaha ya uharibifu

silaha kwa ajili ya kuharibu watu auvitu

silaha ya kuchinja

silaha kwa ajili ya kuchinja watu wengi

tazama!

Neno "tazama" hapa linaongeza msisitizo kwa kinachofuata.

nguo ya kitani

imara, nguo laini iliyo tengenezwa kutokana na mmea. ilivaliwa na watu sehemu ambazo ni moto.

kifaa cha uandishi

vifaa ambavyo waandishi hutumua kuandikia

shaba

chuma kilichopakwa rangi ya dhahabu nyeusi. Imetengezwa na shaba nyekundu sana pamoja kuongezwa chuma kwa uimara.

Ezekiel 9:3

kutoka kwa kerubi ambapo ilikuwa

"kutoka juu ya mabawa manne ya viumbe"

kisingiti cha nyumba

"Nyumba" inarejea kwa hekalu la Mungu.

kitani

imara, nguo laini iliyo tengenezwa kutokana na mmea. ilivaliwa na watu sehemu ambazo ni moto.

kifaa cha uandishi

vifaa ambavyo waandishi hutumua kuandikia

waliolemewa na kushusha/kuvuta pumzi

Hizi ni sauti ambazo watu hufanya wakati wanapojisikia huzuni sana au kusikitishwa kuhusu jambo

machukizo yanafanyika kati ya mji

"mambo ya kutisha yamekuwa yakifanyika katika mji"

Ezekiel 9:5

akaongea na wengine kupitia kusikia

Neno "wengine" linarejea kwa walinzi.

Msiache macho yenu yawe na huruma

"Msiwe na huruma juu ya watu mnaowaona.

msiogope

"msiepuke kuuawa"

alama juu ya kichwa chake

Hawa walikuwa watu waliogugumia kuhusu machukizo yanayotokea katika Yerusalemu.

Anzeni katika patakatifu pangu

"Kuanza kuwaua wale ambao hawana alama katika patakatifu pangu"

wazee

Maana zinazowezekana 1) "wazee sabini wa nyumba ya Israeli" 2) "mzee yeyote"

Ezekiel 9:7

Maelezo ya Jumla:

Mungu anaendelea kunena na walinzi kuwahukumu watu wa Israeli.

kuushambulia mji

"kuwashambulia watu katika mji"

nikaangukia kwenye uso wangu

"nisujudu chini kwenye nchi" au "nikalala kwenye aridhi." Ezekieli hakuanguka kwa ajali. Alienda chini haya kwenye aridhi kuonyesha kwamba alimuheshimu na kumuogopa Yahwe.

Ee, Bwana Yahwe

Ezekieli alisema hivi kwa sababu anataabika sana kwa kile Bwana alichowaambia watu kuifanya Yerusalemu.

je, utayaharibu mabaki yote ya Israeli wakati wa kumwaga ghadhabu yao juu ya Yerusalemu?

"je itawaharibu mabaki yote ya Israeli kwa kumwaga gadhabu yako juu ya Yerusalemu?" Ezekieli anajitetea kwa Yahwe asiwaharibu mabaki.

Ezekiel 9:9

nyumba ya Israeli

Neno "nyumba" ni mfano kwa ajili ya familia iishoyo katika nyumba, katika kesi hii Waisraeli, uzao wa Yakobo zaidi ya miaka mingi.

unaongezeka sana

"kubwa sana"

Nchi imejaa damu

"nchi imejaa udhalimu" au "Nchi yote watu wanawaua watu"

mji umejaa upotovu

"mji umejaa watu wanaofanya mambo ya upotovu."

jicho langu halitatazama kwa huruma

"sitawatazama kwa huruma"

nitaileta juu ya vichwa vyao

"leta madhara ya waliyoyafanya juu ya vichwa vyao." Inamaana "nitawalipa kwa kile walichokifanya"

tazama!

Neno "tazama" hapa linaongeza msisitizo kwa kile kinachofuata.

nguo ya kitani

imara, nguo laini iliyo tengenezwa kutokana na mmea. ilivaliwa na watu sehemu ambazo ni moto.

Alitoa taarifa na kusema

"Alitoa taarifa kwa Yahwe na kumwambia"

Ezekiel 10

Ezekiel 10:1

Maelezo ya Jumla:

Ezekieli anaendelea kueleza kuhusu ono lililoelezwa katika 8:1.

kueleka kuba

"kuelekea paa iliyofunikwa"

kerubi

mnyama mwenye mabawa manne

kama rangi ya samawati

Rangi ya samawati ni jiwe la thamani lenye rangi ya blii au kijani.

mwonekano wake ulikuwa kama kiti cha enzi

"inayofanana kama kiti cha enzi"

mtu aliyevaa nguo ya kitani

imara, nguo laini iliyo tengenezwa kutokana na mmea. ilivaliwa na watu sehemu ambazo ni moto.

Nenda kati ya magurudumu

Tanzama katika sura ya 1:15.

vipande vya mbao vilivyoungua

Hivi ni vipande vya mbao vilivyobaki baada ya moto. Ni vyeusi, vinang'aa rangi nyekundu na chungwa wanapokuwa vyamoto sana.

watawanye juu ya nchi

"wanyunyize juu ya mji" au "watawanye juu ya mji"

Ezekiel 10:3

kerubi

Tazama ilivyotafsiriwa katika 10:3.

upande kuume

inayoelekea mashariki, "upande wa kulia" inaelekea kusini.

utukufu wa Yahwe

Tazama ilivyotafsiriwa katika 1:27.

ukauijaza nyumba

Neno "uka" inarejea kwa utukufu wa Mungu.

Ezekiel 10:6

Ikawa kuhusu

Hili neno limetumika hapa kuonyesha tendo linaanzia wapi.

Mungu alipoamwamuru yule mtu aliyekuwa amevaa nguo za kitani na kusema

Hii inarejea habari iliyokuwa imetolewa katikka 10:1. Baada ya kuchukua kerubi na utukufu wa Mungu katika 10:3-5, Ezekieli anarudi kueleza kuhusu yule mtu aliyekuwa amevalia nguo ya kitani.

yule mtu aliyevalia nguo ya kitani

Tazama maana ya nguo ya kitani ilivyotafsiriwa katika 9:1.

pembeni ya gurudumu

Tazama neno gurudumu lilivyotafsiriwa katika 1:15.

Nikaona juu ya kerubi kitu kama mkono wa mtu juu ya mabawa yao

"nikaona yule kerubi alikuwa na kitu kama mkono wa mtu chini ya mabawa yao"

Ezekiel 10:9

tazama!

Neno "tazama" linaonyesha kwamba Ezekieli alishangazwa kwa kile alichokiona.

magurudumu

Tazama ilivyotafsiriwa katika 1:15.

kerubi

mnyama mwenye mabawa manne

kama jiwe la zabarajadi

"Zabarajadi" ni ngumu sana, jiwe la thamani. Hii zabarajadi ilikuwa ni kama kijani au bluu. Zumaridi ni kijani aina ya zabarajadi na zumaridi ina aina ya bluu ya zabarajadi.

gurudumu linalokingamana na gurudumu jingine

Neno "kingamana" linamaanisha "kukingama" au "kukutana" au "kugusana."

popote kichwa kilipoelekea

"popote kerubi lilipoelekea" au "popote kerubi lilipoelekea"

kichwa

Hii inarejea kwa kichwa cha kerubi lolote.

Ezekiel 10:12

Mwili wao wote

"Miili yote ya kerubi"

magurudumu

Tazama jinsi ilivyotafsiriwa katika 1:15.

magurudumu yalikuwa yakiitwa "kuzunguka."

Neno "kuzunguka." Hapa ni neno la magurudumu. "mtu mmoja aliitwa magurudumu, "kuzunguka'"

Walikuwa na sura nne kila mmoja

"Kila kerubi alikuwa na sura nne" "Kila kiumbe kilikuwa na sura mbele, sura upande wa nyuma, na sura kila upande wa kichwa chake, na sura katika kila upande wa kichwa.

Kerubi

mnyama mwenye mabawa manne

Ezekiel 10:15

kerubi

mnyama mwenye mabawa manne

kiumbe hai

hawa viumbe hai walikuwa na mwonekano wa radi.

Keberi Kanali

Huu ni mto ambao watu katika Kaldayo walichimba kwa ajili ya kumwagilia bustani zao.

kuinuka

"kwenda juu kwenye anga"

Yaliendelea kuwa karibu nao

"Magurudumu yakuwa pamoja na kerubi." "Magurudumu yalihama pamoja na kerubi."

pia yalisimama

"pia yalisimama" au "hayakuhama"

roho wa vile viumbe hai walikuwa kwenye magurudumu

"roho wa viumbe hai aliongoza magurudumu"

Ezekiel 10:18

utkufu wa Yahwe

Tazama ilivotafsiriwa katika 1:17.

nyumba

Inarejea kwa hekalu la Mungu.

"kusimama"

"baki"

simama

Hapa neno "simama" linamaanisha "kusimama" au "kusubiri."

ukaja juu yao kutoka juu

"kwenda juu ya kerubi"

Ezekiel 10:20

viumbe hai

Tazama ilivyotafsiriwa katika 1:13.

Keberi Kanali

Huu ni mto ambao watu katika Kaldayo walichimba kwa ajili ya kumwagilia bustani zao.

alienda mbele

"elekea mbele" au "alitazama kuelekea mbele"

Ezekiel 11

Ezekiel 11:1

Maelezo ya Jumla:

Ezekieli anaendelea kueleza kuhusu ono aliloeleza katika 8:1.

kuelekea mashariki

"inayoelekea mashariki." "Lango la mashariki" iliyoelekea mashariki.

tazama

Neno "tazama" hapa linatutahadharisha kuwa makini kwa habari za kushangaza kwa kinachofuata.

Nyumba ya Yahwe

sehemu ya hekalu

miongoni mwao

"miongoni mwa watu ishirini na tano"

Ezekiel 11:2

Maelezo ya Jumla:

Ezekieli anaendelea kueleza kuhusu maono.

Mwanadamu

"Mwana wa binadamu" Mungu anamuita Ezekieli hivi kusisitiza kwamba Ezekieli ni binadamu tu. Mungu ana uweza na anaishi milele, lakini si watu.

huu mji ni sufuria, na sisi ni nyama

Watu wanajizungumzia wenyewe kana kwamba walikuwa wakataji wa nyama wazuri na mji kana kwamba ulikuwa sufuria ambalo lilihifadhi nyama.

sufuria

sufuria kwa ajili ya kutunzia nyama au sufuria ya kupikia nyama.

Ezekiel 11:5

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na nabii Ezekieli.

Roho wa Yahwe akanijaza

Ezekieli anamzungumzia Roho wa Yahwe kutia moyo na kumtia nguvu kutabiri kana kwamba Roho wa Yahwe amejaa juu yake.

nyumba ya Israeli

Neno "nyumba" ni mfano kwa ajili ya familia, katika kesi hii Waisraeli ambao ni uzao wa Yakobo.

kama unavyosema

"Unanena haya mambo." Hii inarejea kwa kile watu walichokuwa wakikisema katika 11:2.

watu mliowaua ... ni nyama, na huu mji ni sufuria

Yahwe anawazungumzia watu waliouawa kana kwamba walikuwa wakata nyama wazuri na mji kana kwamba ilikuwa sufuria ambayo nyama ilikuwa imehifadhiwa au kupikwa.

Lakini mnaenda kutolewa nje kutoka

"Lakini ninakwenda kuwatoa nje"

Ezekiel 11:8

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa Israeli.

Mmeuogopa upanga, kwa hiyo nauleta huo upanga juu yenu

Neno "upanga" linasimama badala ya adui maadui ambao watashambulia kwa upanga wao.

kuwaweka kwenye mikono ya wageni

Hapa neno "mikono" hapa linawakilisha nguvu au utawala. "nitawawezesha wageni kuwachukua"

Mtaanguka kwa upanga

Neno "upanga" linasimama badala ya adui maadui ambao watawashambulia kwa upanga zao. "Kuanguka kwa upanga" inamaana kwamba watauawa kwa upanga.

mtajua yakwamba mimi ni Yahwe

"mtaelewa kwamba mimi ni Yahwe.

Ezekiel 11:11

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa Israeli.

Huu mji hautakua sufuria yenu ya kupikia, wala hamtakuwa nyama ndani yake

Watu wanajizungumzia wenyewe kana kwamba walikuwa wakataji wa nyama wazuri na mji kana kwamba ulikuwa sufuria ambalo lilihifadhi nyama.

kati ya mipaka

Hii inaonyesha matumizi ya mipaka kuwakilisha Israeli.

mipaka

ukingo wa nje ya nchi au eneo

mtajua ya kwamba mimi ni Yahwe

Tazama katika 6:6

Ezekiel 11:13

Ikawa kwamba

Hili neno limetumika hapa kuonyesha tukio la muhimu katika hadithi.

Pelatia mwana wa Benaya

Alikuwa mmoja wa viongozi waovu wa Israeli aliyetajwa katika 11:1.

ukanijaza kwenye uso wangu

Tazama tafsiri yake katika 1:27.

Ee

Ezekieli anasema hivi kuonyesha hofu yake kuhusu nini kitatokea kwa watu waliosalia huko.

Ezekiel 11:14

Neno la Yahwe likaja

"Yahwe alinena neno lake."

ndugu zako! Ndugu zako!

Hii imetajwa mara mbili kwa msisitizo.

nyumba ya Israeli

Tazama ilivyo tafsiriwa katika 3:1.

Wote hao ndio hao ambao inasemekana wale wanaoishi Yerusalemu

"Watu wanaoishi Yerusalemu wansema kuhusu wote"

Wote hao ndio hao ambao inasemekana

Baadhi ya matoleo ya kisasa yana "Wote ni wale ambao ilisema."

Ezekiel 11:16

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anampatia Ezekieli ujumbe wake kwa Israeli kuhusu wale waliotawanyika.

nimekuwa mtakatifu kwa ajili yao

"nimekuwa pamoja nao kuwalinda."

nchi ambazo walizoend

"mataifa ambayo waliyochukuliwa"

Nitawakusanya kutoka kwa watu, na kuwakutanisha kutoka kwenye nchi

Yahwe amesema hii ahadi mara mbili katika njia tofauti tofauti kwa ajili ya kuonyesha kwamba ni muhimu.

chukizo

"ya kutisha," au "ya kuchukiza"

Ezekiel 11:19

Maelezo ya Jumla:

Mungu anaendelea na unabii wa kile kitakachotokea kwa Wasraeli waliotawanyika.

oyo wa jiwe kutoka kwenye miili yao

Hii ni njia ya kusema kwamba Mungu atabadilisha mwonekano wao kutoka ukaidi wa uasi. "ukaidi wao"

moyo wa nyama

Hii ni njia ya kusema kwamba Mungu atabadilisha mwonekano wao kukubali kanuni yake. "utayari wa kutii"

watatembea kwenye amri zangu, watayachukua maagizo yangu na kuyatenda

Kila moja ya haya maneno inaelezea watu kama kutii kile Yahwe alichowaamuru kufanya.

tabia ya kujifanya

"moyo wa ibaada"

mambo maovu

"mambo ya karaha" au "mambo ya machukizo"

mwenendo

"matendo"

juu ya vichwa vyao wenyewe

"rudi juu ya wale watu."

tamko

"kauli"

Ezekiel 11:22

Maelezo ya Jumla:

Yule kerubi wa Sura ya 10 akaondoka kwenye hekalu na karibu na utukufu wa Mungu.

magurudumu yaliyokuwa karibu nao

Tazama tafsiri yake katika 1:15.

Ezekiel 11:24

uhamisho

"uhamisho" inarejelea kwa Waisraeli walilazimisha kuishi katika Kaldea.

Ezekiel 12

Ezekiel 12:1

Neno la Yahwe likanijia

"Yahwe akanena neno lake."

wana macho ya kuona lakini hawaoni; na wana masikio ya kusikia lakini hawasikii

Haya maneno yote yanatumia pengine macho au masikio kurejea kwa uwezo wa watu kujifunza.

Ezekiel 12:3

Maelezo ya Jumla:

Ezekieli anatekeleza fumbo jingine.

Kwa hiyo wew

"Hivyo hii ni kwa ajili yako"

Labda wataanza kuona, kuwa wao ni nyumba ya uasi

"Pengine wataanza kuelewa kile unacho kieleza" Neno "ona" limetumika kurejea uwezo wa Wayahudi kuelewa.

Ezekiel 12:4

Maelezo ya Jumla:

Mungu ananena na Ezekieli kueleza jinsi atakavyotenda lile fumbo.

katika uso wao

Neno "wao" inarejea kwa watu wa Israeli.

Nyumba ya Israeli

Tazama tafsiri yake katika 3:16.

nimekuweka kama ishara

"nimekuweka kama sahihisho kwa kufikiria kwao"

Ezekiel 12:7

Maelezo ya Jumla:

Ezekieli anawaonyesha watu wa Israeli pundi watalazimika kwenye uhamishoni.

chimba shimo kwenye ukuta kwa mkono

"chimba shimo kwenye ukuta kwa mkono wangu"

nje katika giza

"nje usiku wakati kuna giza"

Ezekiel 12:8

neno la Yahwe likaja

"Yahwe alinena neno lake."

nyumba ya Isaraeli

Tazama tafsiri yake katika 3:16.

Mwanadamu, je nyumba ya Israeli, ile ni nyumba ya uasi, hawakukwambia, 'Unafanya nini?

Mungu anamuuliza hili swali Ezekieli kuonyesha kwamba watu wa Israeli wametangaza kile Ezekieli anachokifanya.

walio kati yao

"walio miongoni mwao"

Ezekiel 12:11

katika giza

"usiku wakati kuna giza"

Nitausambaza wavu wangu juu yake naye atanaswa kwenye mtego wangu

Neno "wavu" na "mtego" yametumika kwa sababu hii ni njia tofauti kukamata mnyama. Mungu anajua kiongozi wa Yerusalemu atafanya nini na ameweka matukio ili kwamba anyakuliwe kama anapojaribu kukimbia.

nitamleta hata Babeli

"nitamfanya achuliwe kwenda Babeli"

Ezekiel 12:14

nitaleta upanga mbele yao

Neno "upanga" limetumika kurejea kwa jeshi la watu wanaobeba panga.

wakati nitakapo watawanya kwenye nchi zote

Haya maneno mawili kimsingi yana maanisha kitu kimoja. "nitakapowafanya wasambaratike kila mmoja na kuishi katika mataifa tofauti tofauti."

kutoka ule upanga

Neno "upanga" linarejea kuuawa katika kupigana.

Ezekiel 12:17

Neno la Yahwe likaja

"Yahwe akanena neno lake."

Mwanadamu

Tazama tafsiri yake katika 2:1.

kula mkate wako kwa kutetemeka, na kunywa maji yako kwa mtetemo na hofu

"ishi maisha yako ya kila siku kwa hofu kubwa." Kula na kunywa ni mambo ya kawaida yanayofanyika katika maisha na hivyo mwambie Ezekieli kuishi kwa hofu kubwa.

Ezekiel 12:19

Watakula mikate yao kwa kutetemeka na kunywa maji yao wakiwa wanatetemeka

Haya maneno mawili yana maana moja na kusisitiza kwamba watu wataogopa sana, hata wakati wa kufanya mambo ya msingi kama kula na kunywa.

miji iliyokuwa wenyeji itahuzunishwa

"huzuni" inaeleza mahali ambapo hakuna mtu anayeishi. "watu katika miji wataondoka au kufa"

mtajua kwamba mimi ni Yahwe

Tazama tafsiri yake katika 6:6.

Ezekiel 12:21

neno la Yahwe likanija

"Yahwe ananena neno lake."

Siku zimerefushwa, na kila ono linaanguka

Huu ulikuwa usemi wa watu wa Israeli ambao hakuamini kwamba Mungu angewahukumu.

Siku zinakaribia

Hili neno linarejea kwa siku ambazo Israeli itahukumiwa.

kila ono litatimizwa

Haya maono Mungu anayoyatoa kwa manabii yatakuwa kweli. "kila unabii utatokea"

Ezekiel 12:24

Maelezo ya Jumla:

Yahwe ananena na watu wa Israeli.

nyumba ya Israeli

Tazama tafsiri katika 3:1.

Hakuna kitu kitakacho chelewesha

"Kile nilicho kitabiri kitatokea punde"

Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo

Tazama taffsiri yake katika 5:11.

nena hili neno

"nena huu ujumbe" au "nena huu unabii"

katika siku zenu

"wakati mkiwa hai"

Ezekiel 12:26

neno la Yahwe likaja

"Yahwe alinena neno lake."

kunijia ... ono ambalo ona ... na ametabiri

Maneno "mimi" na "yeye" yanamrejea Ezekieli.

waambie

Neno "wao" linarejea kwa watu wa Israeli.

Tazama

Neno "Tazama" hapa linatutahadharisha kuwa makini kwa kushangaza habari inayofuata.

'Lile ono alionalo ni kwa siku nyingi kutoka sasa, na ametabiri kipindi kilicho mbali sana

Haya maneno yote ni njia ya watu wa Israeli wanasema maonyo ya Ezekieli hayatatokea katika kipindi cha maisha lakini yatatokea huko mbeleni sana.

Maneno yangu hayatacheleweshwa sana, lakini lile neno nililoliongea litatimizwa

Haya maneno ni njia zote Mungu anawaambia watu wa Israeli kwamba mambo aliyoyaonya, yatatokea punde.

hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo!

Tazama tafsiri yake katika 5:11.

Ezekiel 13

Ezekiel 13:1

neno la Yahwe likaja

"Yahwe alinena neno lake."

mwanadamu

(mimi) Ezekieli

wanotabiri nje ya fikra zao wenyewe

kutabiri kutokana na mawazo yao wenyewe

fuata roho zao wenyewe

Hili neno limetumika kwa nabii kufanya kile wanachotaka. Neno "roho" linarejea kwa mawazo yao na neno "fuata" linarejea kwa kile wanachokifanya.

mbweha

wanyama wa porini kama mbwa au mbweha mwitu.

kama mbeha kwenye aridhi iliyoharibiwa

Kama mbweha aliyeiba chakula kutoka wanyama wengine katika jangwa, manabii huiba kutoka watu wa Israeli wakati wanapodanganya kuhusu kuwa na ujumbe kutoka kwa Mungu.

Ezekiel 13:5

nyumba ya Israeli

Tazama tafsiri yake katika 3:1.

kupinga katika vita

"kujilinda"

Je hamkuwa na maono ya uongo ... Wakati mimi mwenyewe sikuongea?

Yahwe anatumia hili swali kuwakemea manabii wa uongo.

mlikuwa maono ya uongo na kufanya utabiri wa uongo

Tangu manabii wa uongo wakose kupokea ujumbe wa kweli kutoka kwa Yahwe, kile wanacho tabiri kuhusu baadaye sio kweli.

Hivi na hivi

Hili ni nenao lililotumika kurejea kwa kitu chochote nabii ameweza kusema.

Agizo la Yahwe

Tazama tafsiri yake katika 5:11.

Ezekiel 13:8

Maelezo ya Jumla:

Yahwe ananena na watu wa Israeli na kurudia maneno katika njia tofauti tofauti kueleza jinsi walivyo wakweli.

mmekuwa na maono ya uongo na kuwaambia uongo

"mmedanganya kuhusu kuwa na jumbe kutoka kwa Mungu"

Tangazo la Yahwe

Tazama tafsiri yake katika 5:11.

Mkono wangu utakuwa juu ya manabii

Neno "mkono" mara nyingi limetumika katika njia tafauti tofauti kwa uweza wa Yahwe.

mliodanganya maono na wale waliofanya unabii wa uongo

"aliye na jumbe kutoka kwa Mungu lakini anadanganya"

katika kusanyiko la watu wangu, au kuandikishwa katika kumbukumbu ya nyumba ya Israeli

"walio orodheshwa kama watu wangu" Hii ni njia mbili kueleza jambo moja."

nyumba ya Israeli

Tazama tafsiri yake katika 3:1.

mtajua yakwamba mimi ndimi Bwana Yahwe

Tazama tafsiri yake katika 6:6.

Ezekiel 13:10

Kwa sababu hii

Neno "hii" linarejea kwa ahadi ya Bwana kulazimisha manabii wa uongo nje ya Israeli.

wamewaongoza watu wangu

Neno "wao" linarejea kwa manabii wa uongo katika nchi ya Israeli.

wanajenga ukuta ambao wataupaka chokaa

Hapa "ukuta" unasimama kwa ajili ya amani na ulinzi ambao manabii wa uongo wamewaambia watu kwamba Yahwe aliahidi kuwapatia.

kupaka chokaa ... chokaa

"chokaa" ni kimiminika cheupe kilichochanganywa kwa kufanya sehemu ya juu ya kitu (kama vile kuta au wigo)

mvua ya kufurika ... mvua ya mawe ... upepo wa dhoruba

Haya yote ni sehemu ya dhoruba mbaya sana. Mungu anatumia dhoruba kurejea majeshi yatakayoishambulia Yerusalemu.

mvua ya mawe

vigololi vya barafu ambavyo wakati mwingine vinaanguka kutoka angani kipindi cha dhoruba ya mvua.

wengine hawakukwambia

Ezekieli anauliza hili swali kushinikiza jibu.

Ezekiel 13:13

upepo wa dhoruba ... mafuriko ya mvua ... Mvua ya mawe

Hizi sehemu zote ni dhoruba mbaya sana. Mungu anatumia dhoruba kurejea majeshi yatakayoiteka Yerusalemu.

Nitaleta upepo wa dhoruba katika ghadhabu yangu

"wakati nitendapo ghadhabu yangu nitaleta upepo wa dhoruba"

kutakuwa na mafuriko ya mvua kwenye ghadhabu yangu

"wakati nitendapo hasira yangu nitaleta kiasi kikubwa cha mvua"

Mvua ya mawe katika ghadhabu yangu itauharibu kabisa

"Wakati nitendapo juu ya hasira yangu nitaleta mvua ya mawe kuharibu kuta wanaoujenga watu"

kufunua

"isiyofunikwa"

mtaangamizwa

"kuangamizwa kabisa"

kujuwa kwamba mimi ndimi Yahwe

"kutambua kwamba mimi ndimi Yahwe, yule Mungu wa kweli"

Ezekiel 13:15

mimi

inamrejea Yahwe

nitakavo uangamiza kwa ghadhabu yangu

"wakati nitendapo juu ya hasira yangu nitaleta mwisho"

kuupaka chokaa

"kuupaka ukuta rangi nyeupe"

Ukuta hautaonekana tena, wala watu wanaoupaka

"Ukuta hauko huko tena, wala watu"

monoa amani kwa ajili yake

Neno "yeye" inarejea kwa Yerusalemu.

hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo

Tazma tafsiri yake katika 5:11.

Ezekiel 13:17

mwanadamu

Tazama tafsiri yake katika 2:1.

weka uso wako dhidi

Tazama tafsiri yake katika 4:1.

binti za watu wako

wanawake wa Israeli

kutabiri dhidi yao

Hii inamaanisha kuunda unabii kutoka kutokana na fikra zao wenyewe.

hirizi

vitu vilivyoaminika vina nguvu za miujiza.

kutengeza vitambaa vya shela kwa ajili ya vichwa vyao kwa kila kipimo, ili kuwinda watu

Mapambo yaliyovaliwa na manabii yalikuwa kama "mtego" kwa sababu walikuwa wakitumia uzuri, fumbo na uongo kutega watu ili wawaamini na kuasi juu ya Mungu.

Ezekiel 13:19

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunane na juu ya unabii wa uongo katika Israeli.

makonzi ya shayiri na vipande vya mkate

Shayiri ni nafaka iliyotumika kutengenezea mkati na neno "vipande vya mkate" ni kiasi kidogo cha mkate.

Ezekiel 13:20

Bwana Yahwe asema hivi

Tazama tafsiri yake katika 5:5.

hirizi

vitu ambavyo vinavyoaminika vina nguvu ya muujiza

kukamata

"kukamata"

kuyakamata kwa hila maisha ya watu kana kwamba wamekuwa ndege ... watu ambao umewakamata kama ndege

Yahwe analinganisha mapambo ya unabii kukamata kwa ajili ya ndege.

nitazichana kutoka kwenye mikono yenu

Neno "mikono" inarejea inakuja kutawaliwa na unabii. Waongo watatumia utawala wa watu wa Israeli ni kama mikono ambayo imewakamata kurudi kutokana na kukimbia.

havitakamatwa tena katika mikono wako

Kusema hawatakamatwa ni sawa kama kusema watakuwa huru.

kujua kwamba mimi ndimi Yahwe

"kujua kwamba mimi ndimi Yahwe, Mungu wa kweli"

Ezekiel 13:22

mmeuvunja moyo wa mtu mwenye haki

Moyo wa mtu mwenye haki imetumika kurejea kwa hisia zao.

geuka kutoka kwenye njia yake

Kuacha kufanya kitu kinachorejea kurudi katika mwelekeo tofauti.

maono ya uongo au kuendelea kufanya utabiri

Haya maneno yote yanarejea kueleza kuhusu kile kitakachotokea baadaye.

kutokana na mkono wako

Neno "mkono" limetumika kurejea kutawala unabii.

mtajua kwamba mimi ndimi Yahwe

"kutambua kwamba mimi ndimi Yahwe, Mungu wa kweli"

Ezekiel 14

Ezekiel 14:1

neno la Yahwe likaja

"Yahwe alinena neno lake."

wamechukua sanamu zao kwenye mioyo yao

"kufikiria sanamu zao kuwa muhimu sana"

mbele ya nyuso zao

Mungu anasema watu wamehifadhi sanamu ambapo wanaweza kuwaona. Hii inaonyesha sanamu ni muhimu kwao.

pingamizi la uovu wao

Sanamu zinarejea kama kitu dhambi zao zimewafanya kuanguka.

Je naweza kuulizwa yote na wao?

"Hawataniuliza kwa chochote."

Ezekiel 14:4

Kwa hiyo watangazie hivi

Neno "wao" linarejea kwa "watu kutoka wazee wa Isareli"

achukuaye sanamu moyoni mwake

"anayefikiria sanamu zake kuwa muhimu sana"

awekeye pingamizi la uovu mbele ya uso wake

Neno "mbele ya uso waake" inamaanisha "kwa uangalifu mkubwa."

kisha yule ajaye kwa nabii

Mtu aendaye kwa nabii ili kusikia Mungu anasemaje.

idadi ya sanamu zake

"ana kiasi gani cha sanamu."

niweze kuirudisha nyumba ya Israeli katika mioyo yao

"nitawafanya watu wa Israeli wanipende tena"

kuirudisha ... mbali nami

Anasema atawarudisha ili kuwafanya wampende hata kama sanamu zao zimewasukuma mbali na Mungu.

Ezekiel 14:6

nyumba ya Israeli

Tazama tafsiri yake katika 3:1.

Tubuni na rudini kutoka kwenye sanamu zenu! Rudisheni nyuma nyuso zenu kutoka kwenye kachukizo yenu yote

Haya maneno yote ni njia ya kuwaeleza watu wa Israeli kuacha kuabudu sanamu.

Tubuni na rudini

Maneno "Tubu" na "geuka" kimsingi yana maana moja. Kwa pamoja waliimarisha amri ya kuacha kuabudu sanamu.

Ezekiel 14:7

achukuaye sanamu zake kwenye moyo wake

"ambaye afikiriaye sanamu zake kuwa muhimu sana"

na kuweka kwazo la uovu wake mbele ya uso wake mwenyewe

"sanamu ambayo aliyoitumia imetumika kuasi kwa kuiabudu"

nitauweka uso wangu juu ya huyo mtu

"nitakuwa juu yake" au "nitatoa umakini wangu kuwa juu yake"

kumfanya ishara na mithali

Hapa maneno "ishara" na "mithali" yanarejea kwa kitu kinachohifadhi kama kuonya wengine kuhusu matokeo mabaya ya tabia mbaya.

Ezekiel 14:9

Nitanyoosha mkono wangu juu yake

mkono wa Mungu unarejea kwa kile afanyacho. "nitashughulika juu yake"

Watabeba uovu wao wenyewe

"Watawajibika kwa ajili ya kile kibaya walichokifanya"

haitaenda mbali kutoka kunifuata mimi

Neno "mbali kutoka kunifuata" halilingani na kile Mungu anachotaka kwenda mbali naye.

Ezekiel 14:12

neno la Yahwe likanijia

"Yahwe akanena neno lake."

Ezekiel 14:15

hawa watatu

Nuhu, Danieli, na Ayubu

kama niishivyo, asema Bwana Yahwe

"Bwana Yahwe asema. "kama niishivyo"

isipokuwa maisha yao yataokolewa

"Yahwe pekee angeokoa maisha yao"

Ezekiel 14:17

hawa watu watatu

Nuhu, Danieli, na Ayubu

kama niishivyo, asema Bwana Yahwe

"Bwana Yahwe asema. "kama niishivyo"

Ezekiel 14:19

kumwaga ghadhabu yangu

Kama chupa ibebavyo maji, Mungu alikuwa akirudisha hukumu. Hivyo "mwaga ghadhabu yangu" inamaanisha Mungu harudisha tena kutoka kutenda hasira yake lakini atatenda juu ya hasira yake juu ya watu wa Israeli.

kuwakatilia wote mtu na mnyama

Haya maneno yanarejea kuuawa kama tendo la hukumu ya kimungu kwa ajili ya dhambi. "ua wote mtu na mnyama"

Ezekiel 14:21

kutoka kwake

Neno "yeye" inarejea kwa Yerusalemu.

Ezekiel 14:22

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na Ezekieli kuhusu adhabu ya watu wa Israeli.

Tazama!

Neno "Tazazama!" hapa linatutahadharisha kuwa makini kwa habari inayofuata.

salia kwake ... fanya juu yake

Neno "yeye" linarejea kwa Yerusalemu.

njia zao na matendo yao

Maneno haya yote yanarejea kwa kile watu wa Israeli walichokifanya. "vile waishivyo" au "mambo wafanyayo"

Ezekiel 15

Ezekiel 15:1

Maelezo ya Jumala:

Yahwe ananena na Ezekieli katika hii sehemu.

neno la Yahwe likaja

"Yahwe alinena neno lake."

je ni jisni gani mzabibu ulivo bora kuliko mti na matawi yaliyomo kwenye miti katika msitu?

"mzabibu si bora kuliko mti wowote pamoja na matawi ambayo ni miongoni mwa miti katika msitu."

Je watu huwa wanachukua mbao kutoka kwenye mzabbibu kufanyia chochote?

"Watu hawachukui mbao katika mzabibu kufanya chochote."

uwa wanatengenezea kitu kutokana na huo

"hawatengenezi kitu kutoka huo kuning'iniza vitu juu yake."

Kama umetupwa kwenye moto kama kuni, na kama moto umezichoma ncha zake zote na katikati pia, je unafaa kwa chochote?

kama moto ume mwisho wa ncha zake na pia katikati, yamkini sio vyema kwa kitu chochote!

Ezekiel 15:5

Maelezo ya Jumala:

Yahwe anaendelea kuzungumzia kuhusu mzabibu.

Ezekiel 15:7

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na Ezekieli kuhusu watu wa Israeli.

ukiwa

ni mahali ambapo kila mtu ameondoka.

wamefanya dhambi

"wameasi"

hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo

Tazama tafsiri yake katika 5:11.

Ezekiel 16

Ezekiel 16:60

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumrejea Yerusalemu kama mke mzinzi na mataifa mengine kama ndugu wa Yerusalemu.

kumbuka

"kukumbuka"

Ezekiel 16:62

kumbuka kila kitu

"kumbuka kila kitu"

hutafungua mdomo wako tena kusema

"hutasema kitu tena

Ezekiel 17

Ezekiel 17:1

Maelezo ya Jumla:

Ezekieli anasimulia ujumbe ambao aliopewa na Mungu.

Neno la Yahwe likaja

"Yahwe akanena neno lake."

Mwanadamu

Hii inamrejea Ezekieli. Hili neno ni mwanzo wa maneno ya Yahwe aliyoyanena kwa Ezekieli.

tega kitendawili na sema fumbo

"toa fumbo kwao kufikiria"

nyumba ya Israeli

Tazama tafsiri yake katika 3:1.

Tai mkubwa

"tai mkubwa sana"

vipapatio vya kuku, mwenye kujaa manyoya

Neno "kipapatio" linamaanisha mwisho wa nje ya mabawa. "mwishoni mwa mabawa yake kulijawa na mabawa na manyota."

kulikuwa na rangi nyingi

Hii inamrejea tai.

Akakata ncha za matawi

"Akavunja sehemu ndefu sana ya miti"

kuyachukua

"kuchukua sehemu ya juu ya mti" au "chukua matawi"

akaipanda katika mji wa wafanya biashara

Mfanya biashara ni mtu anayeuza vitu.

Ezekiel 17:5

Maelezo ya Jumla:

Huu ni mwendelelzo wa fumbo kuhusu tai.

Pia akachukua

Neno "Yeye" ni tai katika fumbo.

aridhi tayari kwa kupanda

"shamba lililokuwa tayari kwa kupandwa mbegu katika hilo." "aridhi yenye rutba" au "katika aritdhi nzuri."

Aliupanda karibu na maji mengi

"tai alipanda mbegu katika mahali ambapo palikuwa na maji mengi"

kuipanda ... kama mti mti umeao karibu na maji

Miti imeao karibu na maji hukua katika mahali ambapo kuna maji mengi. Kama tai alipanda mbegu kama mti umeao karibu na maji, ina maana kwamba aliupanda katika mahali penye maji mengi.

Kisha ukachipusha

"Kisha mbegu ikaanza kukua kwenye mmea"

mzabibu wenye kutanda

"mzabibu utandao juu ya nchi"

Matawi yake yakamwelekea yeye

Matawi ya mzabibu yakamgeukia tai.

mizizi yake ikamea juu yake

Miziz ya mzabibu ikamea chini ya tai.

Hivyo ukawa mzabibu

"Ambavyo mzabibu humea"

kuzaa matawi na kutoa matawi

"mea matawi na kusambaa mizizi yake"

Ezekiel 17:7

Maelezo ya Jumla:

Utambulisho "lakini" huonyesha kwamba tai mwingine ameelezwa kulikuwa yule wa awali.

tai mkubwa

Tai ni mkubwa, mwenye uwezo, na ndege mwenye kuvutia.

Tazama!

Neno "Tazama" hapa linatahadharisha kuwa makini kwa habari ya kushangaza inayofuata.

Huu mzabibu ukabadilisha mizizi yake kumwelekea tai

"Mizizi ya mzabibu ikamea kumwelekea tai"

upate kumwagiliwa

"hivyo tai akamwagilia mzabibu"

Ulikuwa umepandwa

"yule tai wa awali aliupanda mzabibu."

karibu na kilindi cha maji

"katika mahali ambapo kulikuwa na maji mengi"

hivyo ungezaa matawi na kuanza kutoa matunda, ili kuwa mzabibu mzuri kabisa

"ili mzabibu ukue matawi na matunda na kuwa mzabibu unaovutia"

Ezekiel 17:9

Utafanikiwa?

"Hautafanikiwa."

Je! Haitaing'oa mizizi yake na kuyakata matunda yake ili kwamba unyauke, na majani yake yote mabichi yanyauke?

"Atang'oa mizizi yake na kukonyoa au kuchuma matunda yake hivyo ukuaji wa majani yake yote yatanyauka."

tazama!

Neno "tazama!" hapa inaongeza msisitizo kwa kile kinachofuata. "kuwa macho kwa kile ninachotaka kukueleza!"

utamea?

"hautamea."

Je hautanyauka wakati upepo wa mashariki utakapoupiga?

"Utanyauka wakati upepo wa mashariki uugusapo."

Ezekiel 17:11

neno la Yahwe likaja

"Yahwe akanena neno lake."

Je! hamjui haya mambo yana gana gani?

"Mngetakiwa kujua kwamba hivi vitu nina maana gani."

Tazama!

"Tazama!" au "Sikiliza" au "Kuwa macho kwa kile ninachotaka kukueleza!"

Ezekiel 17:13

ukoo wa kifalme

Neno "ukoo wa kifalme" linawaelezea watu na vitu ambavyo vinavyohusiana na mfalme au malkia.

uzao, muundo wa uzao

"Uzao" ni mtu mwenye uhusiano wa damu moja kwa moja toka kwa mtu mwingine wa mbali katika historia ya familia fulani.

agano

Agano ni makubaliano rasmi, yenye ahadi za viapo baina ya pande mbili ambapo upande mmoja au pande zote zinalazimika kulitimiza.

nadhiri, kiapo, kujiapiza

Katika Biblia, nadhiri ni ahadi rasmi ya kufanya jambo fulani. Mtu anayefanya nadhiri hutakiwa kuitimiza ahadi hiyo. Nadhiri inahusisha mtu kujitoa kuwa mwaminifu na mkweli.

Ezekiel 17:15

Taarifa za Ujumla:

Yehova anazungumza juu ya ufalme wa Yerusalem ulivyoasi dhidi ya mfalme wa Babeli.

Je atafanikiwa?

La hasha ! hatafanikiwa.

Je afanyaye mambo haya atatoroka?

"Afanyaye mambo haya hatatoroka!"

Je ataweza kutoroka Iwapo atalivunja agano?

Iwapo atalivunja agano hatatoroka.

Ezekiel 17:17

Taarifa ya Ujumla:

Yehova anzungumza juu ya mfalme wa Yerusalemu.

Jeshi kubwa na kusanyiko la wengi kwa ajili ya vita.

Vifungu hivi vya maneno kimsingi vina maana sawa na vinasisitiza ni kwa namna gani jeshi la Farao ni kubwa na lenye nguvu.

Hawatamlinda

Hapa neno "hawatamlinda "linarejea kwa mfalme wa Yuda.

Kuta zenye minara

Hii ina maana ya mnara wa wenye ngazi zinazoweza kuwekwa ukutani na kuruhusu wanajeshi kuruka ukuta na kuingia katika mji.

Ezekiel 17:19

Je hiki hakikuwa kiapo changu kwamba alidharau na agano lango alilolivunja?

"kilikuwa kiapo changu kuwa mfalme wa Yerusalemu alidharau na agano langu alilolivunja"

Nitaileta adhabu yake juu ya kichwa chake mwenyewe.

"Nitamuadhibu"

Ataanguka kwa upanga

"atauawa na jeshi la Wababeli"

Ezekiel 17:22

Taarifa za Ujumla:

Yehova anazungumzia juu ya Yerusalemu kana kwamba ni tawi lililopandwa katika milima ya Israeli.

Kuzaa matawi

"yatazalisha matawi mapya"

Ezekiel 17:24

Taarifa za Ujumla:

Yehova anazungumzia juu ya miti kana kwamba ni miji.

Kisha miti yote katika shamba itafahamu kuwa mimi ndimi Yehova.

Vitu kuvikwa uhusika kama binadamu.

Miti mirefu...Miti mifupi

Lugha ya picha/fumbo

Kupukutika

wakati ambapo mmea hunyauka na kufa.

Ezekiel 18

Ezekiel 18:1

Neno la Yehova likanijia

"Yehova alizungumza neno lake." Angalia namna ulivyotafsiri katika 1:1

Mnamaanisha nini, ninyi mnaotumia mithali hii...'wababa wanakula zabibu chachu, na meno ya watoto yametiwa ganzi'

God anawaonya watu kwa kufikiri kuwa wanaadhibiwa kwa dhambi za wazazi wao, lakini wakiamini kuwa wao wenyewe hawana dhambi

Wababa wanakula zabibu chachu, na meno ya watoto yametiwa ganzi

Mithali hii ina maana kuwa watoto wanaadhuibiwa kwa sababu ya matendo maovu ya wazazi wao.

Ezekiel 18:3

Tazama!

Neno "Tazama" hapa linaongeza msisitizo juu ya kile kinachofuata. Linaweza pia kutafsiriwa kama " Haswaa! hii inaweza kutafsiriwa pia kama "ona" au "Sikikiliza" au "zingatia kile ninachoenda kukwambia"

Ezekiel 18:5

Hajakula juu ya milima...hajainua macho yake kuzielekea sanamu

Vifungu hivi vya maneno vinarejea katika ibada ya sanamu. watu walikula chakula ch amatambiko katika vichaka vya mmlima kuzitukuza sanamu. Kifungu cha maneno "kuinua macho yake" ni rejea ya tukio la kuzitazama sanamu na kuzitukuza.

Ezekiel 18:7

alirudisha amana

Mungu anafurahishwa na mkopeshaji anayerudisha amana ya mkopo kwa mkopaji hata kabla ya mkopaji kumlipa mkopeshaji.

Huwapa chakula wenye njaa. Na kuwavika nguo walio uchi.

Mungu anapendezwa na walio wakarimu kwa wasio na chakula na mavazi.

Ezekiel 18:10

humwaga damu

Kifungu hiki cha maneno kinamaanisha kuuwa mtu.

moja kati ya mambo hayo

Hii inamaanisha matendo maovu yaliyotajwa katika 18:11-18:12.

Ezekiel 18:12

Taarifa za Ujumla:

Yehova anaendelea kuzungumza juu ya mwana mkorofi

maskini na wahitaji

Maneno "Maskini" na "muhitaji" yasisitiza kuwa hawa ni watu wasioweza kujisaidia wenyewe.

kutoza riba

Neno "riba" linamaanisha fedha ya nyongeza inayolenga faida juu ya deni.

riba

Neno hili linamaanisha pesa inayolipwa na mtu ili atumie pesa ya mkopo. Hata hivyo baadhi ya tafsiri za leo za neno hilo hutaja kama "riba yoyote" katika kifungu hiki cha maandiko kama "riba kubwa sana"

Ezekiel 18:14

Tazama

Neno "tazama" hapa linaongeza msisitizo juu ya mambo yanayofuata.

tenda

amefanya

Ezekiel 18:16

Taarifa za Msingi:

Yehova anaendelea kuzungumza juu ya mwana asiyetenda dhambi kama za baba yake.

walio uchi

Hii inaweza kumaanisha watu wasio na nguo kabisa, lakini kwa sehemu kubwa inamaanisha watu wenye mavazi chakavu, mavazi duni sana.

huwavika nguo walio uchi

Kuwapatia nguo watu wenye uhitaji wa nguo linazungumziwa kama tendo la kuwavalisha nguo katika miili yao. (lugha ya picha)

huuondoa mkono wake kwa maskini

Hapa neno "mkono" linasimama badala ya maneno "kutenda matendo yasiyo haki"

Ezekiel 18:18

Taarifa za Ujumla:

Yehova anazungumza juu ya baba wa mwana ambaye hajaitii sheria ya Mungu.

kupora

kuchukua kitu cha mtu mwingine kwa kutumia vitisho au mabavu.

tazama

Neno "tazama" hapa linaongeza msisitizo kwa jambo linalofuata.

Ezekiel 18:19

kwanini mwana asibebe uovu wa baba yake?

"kwanini mwana hawajibiki juu ya uovu huo?"

Haki ya kila mtenda mema itakuwa juu yake mwenyewe.

"Kila atendaye kwa haki ataitwa mwenye haki"

uovu wa mtu muovu utakuwa juu yake mwenyewe

"mtu atendaye maovu ataitwa muovu"

Ezekiel 18:21

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anazungumza juu ya mtu muovu anayebadirika na kutenda mema.

kuzingatiwa akilini

"kukumbukwa"

Ataishi kwa haki aitendayo

Ataendelea kuishi kwa sababu anatenda kwa wema"

Ezekiel 18:23

Maelezo ya Jumla:

Yehova anazungumza juu ya shauku yake kwa ajili ya watu waovu.

Je nitafurahia sana juu ya kifo cha mwovu...na si katika kugeuka kwake kutoka katika njia zake mbaya ili aishi?

"sifurahishwi na kifo cha mwovu, bali ninafurahia anapogeuka na kuyaacha matendo yake maovu na akaishi."

Hili ni tamko la Bwana, Yahwe mwenyewe

angalia tafsiri ya 5:11

si katika kugeuka kwake

"asipobadirika na kuyaacha matendo yake maovu na kutenda mema.

Ezekiel 18:24

Maelezo ya Jumla:

Yehova anatoa mfano wa mtu anayegeuka kutoka katika haki na kuugeukia uovu.

je ataishi?

"atakufa tu"

hatazingatiwa akilini

"hatakumbukwa"

Uhaini

kosa ambalo mtu hutenda dhidi ya nchi au dhidi ya Mungu kwa lengo la kusaliti na kujitwalia heshima.

hivyo atakufa katika dhambi anaoutenda

"Hivyo, atakufa kwa ajili yadhambi alizozitenda"

Ezekiel 18:25

kufa kwa sababu ya hayo ... kufa katika alioufanya

Haya maneno yanarudia wazo la mtu anayekufa kwa sababu ya dhambi zake kuonyesha kwamba lilikuwa kosa lake na halikuwa kosa la mtu mwingine yeyote.

Ezekiel 18:27

ameona

ametambua jambo.

Ezekiel 18:29

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kufundisha watu wa Israeli kwa nini njia zake ni za haki.

Je ni namna gani njia zangu haziko sawa, nyumba ya Israeli?

"Huenda njia zangu zi sawa, watu wa Israeli."

Je, ni kwa namna gani njia yako haiko sawa?

"Je, ni namna njia yako i sawa?" "Ni njia yako ambayo

kila mtu miongoni mwenu kulingana na njia zake

"matendo la kila mtu."

ili msiwe

"wao" inarejea kwa makosa ya watu wa Israeli.

Ezekiel 18:31

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na watu wa Israeli.

jifanieni moyo mpya na roho mpya

"kujibadilisha kabisa ulivyo"

nyumba ya Israeli

Tazama tafsiri yake katika 3:1.

hili ni tangazo la Yahwe

Tazama tafsiri yake katika 5:11.

Ezekiel 19

Ezekiel 19:1

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anamweleza Ezekieli kunena na watu wa Israeli.

Ezekiel 19:5

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaenedela kuelezea taifa la Israeli kama simba jike na wafalme wa ufalme wa Yuda kama wanasimba wake.

hivyo alimchukua mwingine miongoni mwa watoto wake

Sasa Yahwe anamlinganisha Yehoyakini na mwana simba mdogo.

Akawakamata wajane na kuiharibu miji

Haya maelezo ni mfano kwa ajili ya Mungu akiruhusu maadui wa Israeli kuyafanya haya mambo.

na viijazvyo

"na kila kitu katika huo"

Ezekiel 19:8

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kulielezea taifa la Isaraeli kama simba jike na wafalme wa ufalme wa Yuda kama wana simba wake.

juu yake

Neno "yeye" linarejea kwa mwana simba mdogo, anayemuwakilisha Yehoyakini.

kutoka mikoa inayozunguka

"kutoka mikoa inayoizunguka nchi ya Israeli."

mikoa

nchi zilizokuwa zimetawaliwa na Babeli

Ezekiel 19:10

mama

Yahwe anaelezea taifa la Israeli ingawa ilikuwa mama wa wana wa Israeli.

mzabibu uliopandwa katika damu yako

"damu" inawakilisha machafuko ya wafalme wa wafalme wa Yuda ambao waliwaua watu.

Ezekiel 19:12

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kulinganisha Israeli na mzabibu na viongozi wake pamoja na matawi imara ya mzabibu.

uliovunjika

"amevunjika"

Ezekiel 19:14

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kulinganisha Israeli na mzabibu na viongozi wake pamoja na matawi imara ya mzabibu.

kutawala

"kwamba mfalme angetumia kutawala"

Ezekiel 20

Ezekiel 20:1

Ikawa

Hili neno limetumika kuonyesha mwanzo wa sehemu ya mwanzo wa hadithi.

katika mwaka wa saba

"katika mwaka wa uhamisho wa Mfalme Yohoyakini"

siku ya kumi ya mwezi wa tano

Hii ni siku ya tano ya mwezi wa kalenda ya Kiebrania. Siku ya kumi ikaribu mwanzoni mwa mwazi wa Nane katika kalenda za magharibi.

mbele yangu

"mbele yangu"

Ezekiel 20:2

neno la Yahwe likaja

"Yahwe akanena neno lake."

Kama niishivyo

Tazama tafsiri yake katika 5:11.

sitaulizwa swali na ninyi

"Sitawaruhusu kuuliza ujumbe wowote kutoka kwangu."

Ezekiel 20:4

Utawahukumu? Utamuhukumu, mwanadamu

"Wahukumu, mwanadamu."

Ulikuwa ukitiririka maziwa na asali

"Nchi yenye wingi wa maziwa na asali ikitiririka." "Ilikuwa nchi yenye rutuba sana."

Ezekiel 20:7

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa viongozi wa Israeli.

kwao

"kwa uzao wa nyumba ya Yakobo"

kutoka mbele ya macho yake

Hili neno lina maanisha kwamba "kwamba anapenda" au "kwamba anaabudu."

Ezekiel 20:8

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa viongozi wa Israeli.

wameasi juu yangu

Neno "wao" linarejea kwa "uzao wa nyumba ya Yakobo."

hawakuwa tayari kunisikiliza

"hawakuweza kunitii"

hivyo haikunajisi katika macho ya mataifa

Hili neno linamaanisha "hivyo mataifa hayatafikiri kwamba jina langu halikuwa takatifu."

walikuwa wakiishi

"walikuwa wakiishi."

Nilijifanya mwenyewe kujulikana kwao

"Nimewaonyesha mataifa mimi ni nani"

katika macho yao

"katika hali yakwamba mataifa wanaweza kuona"

kuwaleta

"kuwaleta watu wa nyumba ya Yakobo"

Ezekiel 20:10

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa wazee wa Israeli.

nimewapeleka

Neno "wao" linarejea kwa "uzao wa nyumba ya Yakobo."

Ezekiel 20:13

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa wazee wa Israeli.

mwaga ghadhabu yangu

Tazama tafsiri yake katika 20:8

nilifanya kwa ajili ya jina langu hivyo lisinajisiwe katika macho ya mataifa

Tazama tafsiri yake katika 20:8.

Ezekiel 20:15

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa wazee wa Israeli.

nimeinua mkono wangu kuapa kiapo

Tazama tafsiri yake katika 20:4.

kwao

"kwa nyumba ya Israeli"

Lakini jicho langu lilikuwa na huruma kwao

"Lakini bado nawahurumia."

kwa sababu ya uharibifu wao

"lakini sikuwaharibu"

Ezekiel 20:18

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa wazee wa Israeli.

Msitembee kama wazazi wenu

"Msifanye mambo ambayo wazazi wenu waliyawaamuru kuyafanya"

msitunze maagizo yao

"msizitii kanuni zao"

tunza maagizo yangu na yatii!

"Kutunza" maagizo ya Yahwe ni sawa na "kuyatii."

mtajua yakwamba mimi ni Yahwe

Tazama tafsiri yake katika 6:6.

Ezekiel 20:21

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa wazee wa Israeli.

Hawakuenenda katika amri zangu

Tazama tafsiri hii katika 20:13.

hivyo nimeamua kumwaga ghadhabu yangu juu yao kutimiza ghadhabu yangu

Tazama hii tafsiri katika 20:8.

Ezekiel 20:23

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa wazee wa Israeli.

nimeuinua mkono wangu kuapa juu yao

Ilikuwa ni mazoea ya kawaida kuapa kiapo kwa kuinua mkono kuelekea mbinguni.

nitawatawanya kati ya maifa na kuwatawanya miongoni mwa nchi mabali mbali

Tazama tafsiri hii katika 12:14.

Macho yao yalizitamani sanamu za baba zao

"walikuwa na shauku ya kuabudu sanamu ambazo wazazi wao walizoziabudu."

Ezekiel 20:25

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa wazee wa Israeli.

Kisha niliwapa amri ambazo hazikuwa nzuri, na maagizo ambayo hawakuweza kuishi kwayo

Maneno amri katika hili neno halirejelei sheria ya Mungu. Mungu aliwaruhusu kuishi kwa sheria ya mwanadamu na hukumu ambazo hazikuwa nzuri.

kuwapatia

Neno "wao" linarejea kwa watoto ambao Yahwe aliwatoa Misri.

kwa zawadi zao

"kwa zawadi ambazo walizokuwa wamenipatia."

waweke kwenye moto

Hii inamaanisha kutoa sadaka mtoto kwa sanamu kwa kuwachoma wakiwa hai.

Ezekiel 20:27

Nini maana ya mahali palipoinuka ambapo mmeleta sadaka huko

"Hii ni mahali pa juu ambapo unatakiwa kuleta sadaka!"

jina lake linaitwa Bama

"Watu wemeiita hapo mahali Bama" "Bama" maana yake "mahali pa juu," mahali kwa ajili kuabudu sanamu.

Ezekiel 20:30

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa njumba ya Israeli.

weka wana wako kwenye moto

Hii inamaanisha kutoa sadaka watoto kwa sanamu kwa kuwachoma wakiwa hai.

Hivyo kwa nini nikuache unihoji mimi ... Israeli?

"Hauna haki ya kuniuliza ujumbe ... Israeli."

Ezekiel 20:33

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa nyumba ya Israeli.

mkono wenye nguvu, mkono ulionyooshwa

Maneno haya yote yanarejea kwa uweza mkubwa.

Ezekiel 20:36

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa nyumba ya Israeli.

Ezekiel 20:39

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa nyumba ya Israeli.

nyumba ya Israeli

Tazama jinsi ya kutafsiri hii katika 3:1.

kunisikiliza

"kunitii" au "kuvuta usikivu kwangu"

Ezekiel 20:40

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa nyumba ya Israeli.

kutaka

"kulazimu kuleta"

malimbuko ya kodi zenu

Hapa "malimbuko" huenda inamaanisha vitu bora miongoni mwa sadaka zote zilizowekwa pembeni kutoa kwa Mungu.

vitu vyako vitakatifu

"sadaka ulizoziweka pembeni kunitolea"

nitakapowatoa kutoka wale watu na kuwakusanya toka nchi ambazo mlizotawanyika

Haya maneno mawili yanamaanisha kitu kimoja na kusisitiza kwamba Yahwe atawarudisha watu wake kutoka mataifa yote ambayo aliyokuwa amewatawanya.

mlikuwa mmetawanyika

"nimewatawanya."

Nitajifunua mimi mwenyewe kama mtakatifu ndani yenu kwa ajili ya mataifa waone

"nitakutumia kuonyesha mataifa kwamba mimi ni mtakatifu"

Ezekiel 20:42

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpataia Ezekieli ujumbe wake kwenye nyumba ya Israeli.

inua mkono wangu

Hili neno linamaanisha "nimeapa" au "nimeahidi."

mtajua kuwa mimi ndimi Yahwe

Tazama tafsiri yake katika 6:6.

hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.

Tazama tafsiri yake katika 5:11.

Ezekiel 20:45

neno la Yahwe likaja

"Yahwe akanena neno lake."

Ezekiel 20:48

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwenye msitu wa Negevu.

wataona

"wataelewa"

Ee

neno linaloonyesha kuteseka au huzuni

e! yeye sio mwenye kusema mafumbo?

Anaeleza hadithi"

Ezekiel 21

Ezekiel 21:1

Mwana wa adamu

"Mwana wa mwanadamu" Mungu anamuita Ezekieli hivi kusisitiza kwamba Ezekieli ni mwanadamu tu. Mungu ana uwezo na huishi milele, lakini watu hapana.

neno la Yahwe likanijia

"Yahwe akanipatia ujumbe."

weka uso wako kulekea Yerusalemu

Hii ni lahaja. Hii inamaanisha kwamba Yahwe anatupa hukumu juu ya Yerusalemu na kunena hukumu juu yake.

Nitautoa upanga wangu kutoka kwenye ala yake na kuwakatilia mbali wote yaani mtu mwenye haki na mtu mwovu kutoka kwako

Hii inazungumzia Yahwe akiwafanya hawa watu kufa kana kwamba amewaua kweli kwa upanga wake mwenyewe.

mtu mwenye haki na mtu mwovu kutoka kwako!

watu wenye haki na watu waovu." Hii inarejea kwa watu wengi, sio mtu mmoja menye haki na mtu mmoja mwovu.

ala

kitu kinachoshikilia na kufunika upanga wakati unapokuwa hautumiki

katilia mbali

Hii inamaanisha kuua "ua"

Ezekiel 21:4

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe kwa nchi ya Israeli.

katilia mbali

Hii inamaanisha kuua "ua"

mwenye haki ... mwovu

Hii inarejea kwa watu wenye haki na waovu. "wale ambao ni wenye haki ... wale walio waovu" au "watu wenye haki ... watu waovu"

kutoka kwako

"miongoni mwako"

upanga wangu utatoka kutoka kwenye ala yake dhidi ya

Hii inamzungumzia Yahwe akifanya hawa watu kufa kana kwamba amewau hasa kwa upanga wake mwenyewe.

wenye miili wote

Hapa "mwili" ni mfani kwa "watu" "watu wote"

kutoka kusini kwenda kaskazini

Hii inarejea kwa eneo la kaskazini, na kusini, na maeneo yote ya katikati. "katika kila uelekeo" "kila mahali"

kwamba mimi, Yahwe, nimeutoa upanga wangu kutoka kwenye ala yake

Hii inamwongelea Yahwe akisababisha watu kufa kana kwamba amewaua kweli kwa upanga wake.

Hautarudi tena

Hii inamzungumzia Yahwe haurudishi upanga wake kutoka kuwashambulia watu kana kwamba upanga ulikuwa mtu ambaye hakuwa ameshikilia upanga wenyewe kuurudisha kutoka kushambulia.

Ezekiel 21:6

Maelezo ya Jumla:

Yahwe ananena na Ezekieli.

mwana wa adamu

"mwana wa mwanadamu"

gumia kama kuvunjika kwa viuno vyako

Yahwe anamwambia Ezekieli kugugumia kama ishara ya kuusindikiza ujumbe wake. Anamwambia kugugumia kwa kina kana kwamba tumbo lake lilikuwa kwenye maumivu makubwa sana.

Katika uchungu wa gumia

"Kwa huzuni kubwa"

mbele ya macho yao

Hapa Waisraeli wanarejelewa kwa "macho" yao kusisitiza kile wakionacho. "mbele yao" au "mbele ya watu wa Israeli"

ile habari inayokuja

Hii inazungumzia "habari" kana kwamba ilikuwa mtu ambaye alikuwa akija kwao punde.

kwa kila moyo utakaozimia

Hii inazungumzia watu kuogopa kana kwamba mioyo yao ilikuwa ikizimia.

utasita

"utakuwa dhaifu"

Kila roho itazimia

Hii inazungumzia watu kuwa na hofu katika roho zao kana kwamba roho zao zilitaka kuzimia.

kila goti litatiririka kama maji

"kila goti litakuwa dhaifu kama maji"

Ezekiel 21:8

neno la Yahwe likaja

"Yahwe ananena neno lake."

Utachongwa na kung'aa

"Li kali na lililosuguliwa." Hili neno linaonyesha kwamba upanga u tayari kwa ajili ya mtu kuutumia.

kung'aa

Mtuu kuufanya upanga laini, unaong'aa, na safi kwa kuusugua kwa kwa kifaa kinacho kwaruza

Ezekiel 21:10

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa watu wa Yerusalemu na wa nchi ya Israeli.

Utanolewa ... utang'arishwa ili

"nitaunoa ... nitaunoa ili kwamba uta"

ili uwe kama mng'ao wa radi

Hii inamaanisha kwamba utang'aa sana huo mwanga utaakisi na kung'aa. "Hivyo utawaka kama nuru"

Je! Tufanye furaha katika fimbo ya mwana wa mfalme?

Hili swali lisilohitaji majibu linasisitiza kwamba watu wa Israeli hawatasheherekea uwezo wa ufalme wao, kwa sababu hautaweza kuupitisha "upanga."

Tuta

Neno "sisi" linamrejea Ezekieli na watu wa Israeli.

katika mwana wangu wa kifalme

Hapa Yahwe anarejea kwa mfalme wa Yuda kama mwana wake. Fimbo ya mfalme inawakilisha utawala wake kama mfalme.

Upanga ujao huchukia kila hiyo fimbo

Hapa neno "upanga" Hii inazungumzia mfalme kutoweza kuupitisha "upanga" kama "upanga" unauichukia fimbo ya mfalme.

hiyo fimbo

Hili neno limetumika kuidhihaki fimbo ya mfalme kwa kuiita "fimbo." "hiyo fimbo"

upanga utatolewa kung'arishwa

"nitaung'arisha upanga"

kisha kushikika kwa mkono

"kisha mtu sahihi ataushika katika mkono wake"

utatolewa kwenye mkono wa yule auaye

"u tayari kwa ajili ya matumiziya kuua"

Ezekiel 21:12

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe kwa watu wa Yerusalemu na nchi ya Israeli.

Wametolewa dhidi ya upanga pamoja na watu wangu

"Wameuawa kwa upanga pembeni ya watu wangu"

lakini itakuwaje kama fimbo ya kifalme haitakuwepo tena?

"na itakuwa hofu kubwa sana kama upanga utaiharibu fimbo na fimbo ikaenda."

Ezekiel 21:14

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia ezekieli ujumbe wake.

Upanga kwa wale watakaochinjwa

"Upanga kwa ajili ya kuchinja watu."

ukiwatoboa

Neno "wao" linarejea kwa watu wa Yerusalemu na wa nchi ya Israeli.

Ezekiel 21:15

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa watu wa Yuerusalemu na wa nchi ya Israeli.

kuongeza kuanguka kwao

Hapa "kuanguka" inarejea kwa watu kuuawa katika vita. "kuwaua watu miongoni mwao"

malango yao

Neno "yao" inarejea kwa watu wa Yerusalemu.

Wewe, upanga! Nyooka upande wa kuume! ...Nenda popote ulipoelekeza uso wako

Ipo kama Yahwe alikuwa akinena na upanga.

popote ulipoelekeza uso wako

"Popote nilipoelekeza ubapa wako."

uso wako

Hapa "uso" inasimama kwa ajili ya makali ya upanga.

Ezekiel 21:18

Neno la Yahwe likaja

"Yahwe akanena neno lake."

mwana wa adamu

Tazama tafsiri ya hii katika 2:1.

upanga

"vita."

Ezekiel 21:21

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake.

mitambo ya kubomolea

mashine kubwa ambazo watu walizitumia kuangusha chini kuta au minara

juu yake

"juu ya Yerusalemu

kujenga ngazi

Hizi zilikuwa ngazi kubwa ambazo mfalme wa babeli alizijenga ili kwamba maaskari wake waweze kuingia kwenye kuta za Yerusalemu.

minara ya boma

Hii ilikuwa minara ya mbao ambayo mfalme wa Babeli aliijenga kuzunguka Yerusalemu kuwawezesha maaskari wa Babebli kurusha mishale juu ya kuta za Yerusalemu.

Ezekiel 21:24

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa watu wa Yerusalemu.

Kwa sababu umeuleta uovu wako kwenye kumbukumbu zangu

"Kwa sababu umenikumbusha uovu wako"

uovu wako kwenye kumbukumbu zangu, makosa yenu yatafunuliwa! Dhambi zenu zitaonekana katika matendo yenu yote

"kwa kuufunua uovu wako, dhambi zako zitaonyeshwa wazi kwa kila mtu."

Kwa sababu hii utamkumbusha kila mtu kwamba

"Kwa sababu hii kila mtu ataelewa kwamba"

utatekwa kwa mkono wa adui zako

"mfalme wa Babeli atakuteka."

Ezekiel 21:25

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anampatia Ezekieli ujumbe wake kwa mtwala wa Israeli.

siku ya nani inakuja

Hili neno linamaanisha "sasa Yahwe atamwadhibu nani."

mda wa nani wa kufanya dhambi umekoma

"mda wakati Yahwe akomeshapo uovu"

kilemba

kipande cha nguo kizuri ambacho mfalme huvaa kwenye vichwa vyao kama ishara ya mamlaka yao

tukuza unyenyekevu

"na tukuza ya chini"

Ezekiel 21:28

mwana wa adamu

Tazama tafsiri yake katika 2:1.

umetolewa

"umtolewa nje ya ala yake"

Wakati manabii waonapo maono kwa ajili yako

Neno "wew" inarejea kwa taifa la Amoni.

maono matupu

"maono ya uongo"

Ezekiel 21:30

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa watu wa Amoni.

ala

tazama tafsiri yake katika 21:1.

Katika mahali pako pa uumbaji

"Katika mahali ambapo nilipo kuumbia"

Ezekiel 21:32

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa watu wa Amoni.

Utakuwa kuni kwa ajili ya moto

"Moto utakuchoma"

Ezekiel 22

Ezekiel 22:1

neno la Yahwe likaja

"Yahwe akanena neno lake."

Sasa wewe, mwanadamu, Je! Utanihukumu? Utauhukumu mji kwa damu?

"Mwana wa adamu, nenda kahukumu. Nenda na uhukumu mji wa damu."

mji wa damu

Yahwe anarejea kwa Yerusalemu kama mji wa damu. Hii inarejea kwa wauaji na machafuko yaliyotokea katika Yerusalemu.

yeye ... yeye mwenyewe

Neno "yeye" linairejea Yerusalemu. Miji ilikuwa ikifikiriwa kama mwanamke. Hii inaendelea hadi mstari wa 32.

Ezekiel 22:4

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaenedela kunena na Ezekieli kwa watu wa Yerusalemu.

Kwa kuwa umezileta karibu siku zako na kuzikaribia miaka yako ya mwisho

Maneno haya yote yanamaanisha kwamba wakati mda Yahwe atakapoiadhibu Yerusalemu u karibu.

kujaa machafuko

watu wengi katika Yerusalemu wamechanganyikiwa

Ezekiel 22:6

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anazungumzia kuhusu mtawala wa Israeli katika Yerusalemu.

Tazama

"Tazama" au "Sikia" au "Vuta usikivu kwa kile ninachotaka kukwambia."

wamekuja kwako ... kati yako

Hili neno "wewe" na "yako" inarejea kwa Yerusalemu.

wamekula kwenye milima

Hapa "milima" linarejea kwa madhabahu kwa sanamu ambazo zi juu ya milima. Wakala nyama ambazo zilizokuwa zimetolewa kwa sanamu kwa ajili ya kuwa na baraka ya miungu.

Wamefanya uovu kati yako

Hii inamaanisha kwamba wanafanya mambo maovu ndani ya mji wa Yerusalemu.

Ezekiel 22:10

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na Ezekieli kupitia Ezekieli kuhusu mambo mabaya ambayo watu wa Yerusalemu waliyoyafanya.

ninyi ... wao

Hivi viwakilishi majina vinarejea kwa Yerusalemu (watu wa Yerusalemu).

Uchi wa baba umefunuliwa

Huyu ni mke wa baba. Ni uchi ambao unaomaanisha kwa yeye kuona.

Wamemtukana ... waliofanya machukizo pamoja ... kuwafanya uchafu wa aibu kwa mke wa mwanao mwenyewe

uchafu wa aibu - Hizi ni njia zote za kueleza kwamba wanaume wamelala na wanwake ambao hawakutakiwa na jinsi matendo yao ya dhambi yalivyo.

vutia

Hili neno linarejea kwenye pesa zilizolipwa na mtu kutumia pesa iliyoazimwa. Ingawa baadhi ya baadhi ya matoleo ya kisasa yanatafsiri "kuvutia" katika kifungu hiki kama "kuvutia sana."

umenisahau

kukataa kumtii Yahwe ni kama kusahau kwamba anaishi.

Ezekiel 22:13

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na watu wa Yerusalemu kwa kunena moja kwa moja na mji wa Yerusalemu.

nimeipiga faida mdanganyifu ... damu

Neno "piga" linarejea kwa Yahwe kuchukua uamuzi juu ya hivi vitu.

e! Moyo wako utasimama, mikono yako itakuwa hodari katika siku wakati mimi mwenyewe nitakapo kushughulikia?

"Moyo wako hautasiamama, mikono yako haitakuwa imara katika siku wakati mimi nitakapo shughulika na wewe.

nitakutawanya kati ya mataifa na kukutawanya kati ya nchi mbali mbali

Tazama tafsiri yake katika 12:14.

safisha

toa kitu ambacho hakitakiwi.

katika macho ya mataifa

"katika wazo la watu katika mataifa mengine"

Ezekiel 22:17

neno la Yahwe likaja

"Yahwe akanena neno lake."

takataka

"haina thamani"

Wote wamekuwa masazo ya shaba na bati, na chuma na risasi kati yenu

"Watu wote waliokuzunguka hawana thamani"

Ezekiel 22:20

Maelezo ya Jumla:

Mungu anaendelea kueleza adhabu yake ya watu kama Yerusalemu kama vitu vilivyokuwa vimeyeyushwa na kusafishwa katika tanuu.

Nitakuyeyusha

Adhabu ya Mungu inarejewa kama moto wa tanuu unaoisafisha Yerusalemu kama tanuu inayoisambaratisha vifaa isiyo na thamani kutoka vifaa vyenya thamani wakati wanapoiyeyusha.

Ezekiel 22:23

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anamwambia Ezekieli kunena na Yerusalemu.

Neno la Yahwe likaja

"Yahwe akanena neno lake."

Hakuna mvua katika siku ya ghadhabu

Mvua imetumika kama mfano wa baraka ya Mungu. "Hakuna baraka katika siku ya ghadhabu"

njama

mpango wa siri wa watu wawili au zaidi kufanya kitu kiumizacho au kuvunja sheria.

Ezekiel 22:26

yeye

Hiki kiwakilishi cha jina kinarejea kwa Yerusalemu.

Wamemwaga damu na kuharibu maisha

Haya maneno mawili kimsingi yanamaanisha kitu kimoja na kusisitiza machafuko ambayo wana mfalme wa Yerusalemu wanayoyafanya. "Wanawaua watu"

Ezekiel 22:30

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anawalinganisha viongozi wa Yerusalemu kwenye ukuta na yeye mwenyewe kwa kushambilia jeshi.

mtu kutoka kwao ambaye ataweza kujenga ukuta

kiongozi akijikabidhi yeyey mwenyewe kati ya Yahwe na watu kwa kuchukua wajibu kuwaongoza kurudi kutoka kwenye haki. "mtu kutoka kwao ambaye ataweza kufanya kama ukuta"

kusimama mbele yangu katika uvunjaji wake

kusimama katika mahali ukuta ulipo vunjika. Kiongozi anawatetea watu wa Israeli ni kama shujaa kuutetea mji katika vita.

nitaimwaga ghadhabu yangu juu yao!

huku itakayoweza kumwagwa kama maji kutoka kwenye bakuli.

moto wa ghadhabu yangu

hukumu ya Mungu ni kama moto kwa sababu ni kali sana.

weka njia zao katika vichwa vyao wenyewe

Kuweka kitu juu ya kichwa cha mtu inarejea kwa kuwafanya kuibeba au kuchukua wajibu kwa kuweja juu yake. "wafanye kuchukua wajibu kwa kile walichokifanya"

Ezekiel 23

Ezekiel 23:1

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anamwambia Ezekieli hadithi kuhusu mabinti wawili katika Misri kuelezea jinsi alivyoona tabia ya watu wa Israeli.

Neno la Yahwe likaja

"Yahwe akanena neno lake."

maziwa yao yalikuwa yamebanwa

"Wanaume waliyabana maziwa yao."

ubikira wa chuchu zao zilipapaswa huko

Kimsingi haya maneno yanamaanisha kitu kimoja kama neno lililopita na kusisitiza tabia mbaya ya wasichana wawili.

papaswa

kushikwa pole pole

Ohola

Hili ni jina la kike linalomaanisha "hema yake."

Oholiba

Hili ni jina la kike linalomaanisha "hima yake yu katikati yake."

Ezekiel 23:5

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendela kumweleza Ezekieli hadithi yake kuhusu uznifu wa mke wake Ohola.

nguvu

"katika utawala"

watu bora wote wa Ashuru

Hii inatambulisha mwenye neno "wao" inarejewa kwa.

Ezekiel 23:8

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumweleza Ezekieli kuhusu uzinifu wa mke wake Ohola

wakati walipoanza kummwagia tabia ya uzinzi

Neno "mwaga" linatumia wazo la maji kumwagwa kueleza kitu kikitokea katika mlima mkubwa.

kwenye mkono wa mpenzi wake, kwenye mkono wa Waashuru

Neno "mkono" linarejea kwa nguvu au mamlaka. Neno la pili linaeleza kwamba "wapenzi wake" walikuwa "Waashuru."

Ezekiel 23:11

Maelezo ya Jumla:

Yahwe akaanza kumweleza Ezekieli kuhusu uzinifu wa mke wake Oholiba, dada yake na Ohola.

Oholiba

Hili ni jina la kike linalomaanisha "hima yake yu katikati yake."

waliokuwa wamevaa ngua za ushawishi, walikuwa watu waendesha farasi

Maneno haya yote yanaelezea watu ambao ni matajiri. "waliokuwa matajiri"

Ilikuwa kama kwa dada wote

"Dada wote wakawa najisi kupitia matendo yao ya ukahaba"

Ezekiel 23:14

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kueleza hadithi kuhusu mke wake mzinifu Oholiba kwa Ezekieli.

vilemba

chepeo zilizotengenezwa kwa nguo ndefu na kufunika juu ya kichwa cha mtu.

Ezekiel 23:16

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kueleza hadithi kuhsu mke mzinifu Oholiba kwa Ezekieli.

basi akageuka mwenyewe kutoka kwao katika karaha

"mohemko yake kuhusu wao ilibadilika kutoka kutamani hata karaha"

Ezekiel 23:18

akakumbuka na kutafakari siku za ujana wake

"kumbuka na kufanya vitu vile vile kama alivyokuwa amefanya wakati alipokuwa kijana"

Ezekiel 23:20

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anamalizia kuzungumzia kuhusu Oholiba na Waashuri na kuanza kuzungumza na Oholiba.

ambao sehemu zao za siri zilikuwa kama zile za punda, na kile kizaliwacho hutoka kilikuwa kama wale farasi

ili kuonyesha jinsi Oholiba alivyokuwa na tamaa ya kutamani.

Ezekiel 23:22

Tazama

"Ona" au "Sikiliza" au "Kuwa makini kwa kile ninachotaka kukuambia."

Pekodi, Shoa, na Koa

Haya ni makundi ya watu waliooshi Babeli.

Ezekiel 23:24

sialaha

Neno la Kiebrani hapa limetafsiri kama "silaha" ni adimu. Matoleo mengi ya kisasa yanaitafsiri katika njia hii, lakini baadhi ya matoleo yameiacha kama ilivyo.

Watapanga ngao kubwa, ngao ndogo, na kofia za chuma juu yako

Hizi njia za utetezi zimetumika kurejea kwa aina tofauti tofauti za maaskari katika jeshi.

Wataikata pua yako na maskio yako

Hii inaelezea adhabu katika Babeli kwa mwanamke aliyeoolewa ambaye alilala na wanaume ambao sio waume zao. "Watawaadhibu kama wazinzi"

Ezekiel 23:26

Hutayainuja macho yako

Hii ni njia ya kumrejea mtu kugeuza kichwa chao kutazama kitu. "Hutaona"

hutaikumbuka Misri tena

Hili nenao "fikiria Misri" linarejea kwa matendo ya kikahaba aliyojifunza katika Misri. Hatawafikiria tena kwa sababu amejifunza hawatampatia vitu vizuri ambavyo Wamisri, na Waashuru walivyonavyo. Badala yake, matendo ya kikahaba vimemsababisha yeye kuadhibiwa na hatataka kufikiria kuhusu kuwafanya tena.

Ezekiel 23:28

Tazama

Neno "tazama" hapa linamalizia kusisitiza kile kinachofuata.

uchi na kuweka wazi

Haya maneno mawili yanamaanisha jambo moja na kusisitiza kwamba atakuwa uchi kabisa.

tabia yako ya aibu na uzinzi wako

Haya maneno yote yanaelezea ukahaba wake na kusisitiza jinsi tabia yake hii ilivyokuwa mbaya.

Ezekiel 23:30

umetenda kama kahaba, tamaa za mataifa

Oholiba anatenda kama kahaba pamoja na mataifa kwa sababu wanaume aliolala nao ni alama ya utajiri na nguvu ya haya mataifa.

nitakiweka kikombe chake

Neno "kikombe" linajea kwa hukumu ya Oholiba. Inawakilisha kitu alichokipokea.

Ezekiel 23:32

Utakinyea kikombe cha dada yako

Kunywa kutoka kikombe kimoja ni njia nyingine ya kusema watazoea jambo moja. "Utazoea hukumu ileile kama dada yako"

ambacho ni kirefu na kikubwa

Hii inarejea kwa kiasi cha hukumu kilichopokelewa. "hiyo ni kali"

dhihaka ... kitu kwa ajili ya dhihaka

maneno haya yoye yanarejea kwa mtu anayechekwa na

kikombe kimejaa kiasi kikubwa

Hii sentensi haisemi nini kilichopo katika kakombe kwa sababu imeeleweka kwa kusoma 23:30.

Ezekiel 23:33

kikombe cha ushangao na uharibifu

"kikombe kinachosababisha mshangao na uharibifu." neno "uharibifu" na "mshangao yanashirikiana maana moja hapa na kusisitiza jinsi hukumu yake itakavyokuwa ya kutisha.

kikombe cha dada yako Samaria

Oholiba dada yake na Ohola amewakilisha Samaria. Samaria imeitwa kwa jina lake lakini bado inarejelewa kama dada. Kikombe ni ishara ya adhabu aliyoipokea.

hivyo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo

Tazama jinsi ya ilivyotafsiriwa katika 5:11.

Ezekiel 23:35

na kunitupa mbali nyumba ya mgongo wako

Yahwe anasema Oholiba hajali kuhusu yeye.

Ezekiel 23:36

Mwanadamu, Je! utamhukumu Ohola na Oholiba?

"Mwanadamu, utamuhumu Ohola na Oholiba!"

kuna damu juu ya vichwa vyao

Damu ni matokea ya kuwaua watu, na kwa hiyo inawakilisha mauaji. "Wamewaua watu."

Ezekiel 23:38

Maelezo ya Jumla:

Yahwe ananena na Ezekieli kuhusu Ohola na Oholiba.

na katika siku hiyo hiyo wakainajisi Sabato zangu

Neno "siku hiyo hiyo" linarejea kwa neno lililopita "fanya patakatifu pangu najisi." "na juu ya siku hiyo hiyo wamepafanya patakatifu pangu najisi, wamezinajisi Sabato zangu"

wakaja hata patakatifu pangu siku hiyo hiyo kupanajisi

"wakaja kupanajisi patakatifu pangu siku hiyo hiyo wakiwachinja watoto wao kwa ajili ya miungu yao"

tazama!

Neno "tazama" hapa linaongeza msisitizo kwa kile kifuatacho. "hasa!"

Ezekiel 23:40

Maelezo ya Jumla:

Ezekieli ananena na Ohola na Oholiba.

tazama!

"tazama" au "sikiliza" au "kuwa makini kwa kile ninachotaka kukueleza!"

uliojiosha kwa ajili yao, uliweka rangi macho yako, na kujipamba kwa mapambo ya vito

Haya mabo yalifanywa na mwanamke mmoja kumfanya aonekane mrembo zaidi kwa mwanamume.

ubani wangu na mafuta yangu

vitu vilivyotumika katika kumwabudu Yahwe.

Ezekiel 23:42

sauti za kundi la watu waliokuwa pamoja na wapiganaji zilikuwa pamoja nawe

Sauti za kundi la watu imetumika kurejea kwa kundi la watu.

walevi

watu ambao mara nyingi hulewa. Ingawa baadhi ya matoleo ya kisasa yanatafsiri Washeba," ambayo ni, watu kutoka Sheba.

mapambo

pamba au kuchonga kufanya nzuri zaidi.

Ezekiel 23:43

juu yake aliyekuwa ameonywa kwa uzinzi

juu yake aliyekuwa ameonywa kwa uzinzi -Ezekieli anarejea kwa Ohola na Ohobila pamoja na maelezo.

walivyokuwa kama kahaba yeyote

"walipokuwa wakimpenyeza kahaba yeyote"

wana damu juu ya vichwa vyao

Hili neno linatumia ushahidi wa nguvu kusema wana nguvu ya hatia.

Ezekiel 23:46

inua kundi la watu

Hili neno "inua" linarejea kuongeza hesabu ya watu. "kusanya kundi kubwa la watu"

kuwatoa

Yahwe anatoa wajibu kuwaangalia na kuwaruhusu kutaabika kwa uchaguzi wao.

kuwa kitisho na kuteka nyara

"kwa kundi kutisha na kuwateka nyara."

Ezekiel 23:48

weka tabia yenu ya aibu juu yenu

"kuwafanya kukubali majukumu kwa ajili ya tabia zenu za aibu"

chukua hatia ya dhambi zenu

"kubali majukumu kwa ajili ya hatia ya dhambi zenu"

Ezekiel 24

Ezekiel 24:1

Maelezo ya Jumla:

Yahwe ananena na Ezekieli.

Neno la Yahwe likanijia

"Yahwe akanena neno lake."

katika mwaka wa tisa

"katika mwaka wa tisa wa uhamisho wa Mfalme Yehoyakini"

mweziwa kumi, na katika siku ya kumi ya mwezi

"siku ya kumi ya mwazi wa kumi." Huu ni mwezi wa kumi wa kalenda ya Kiebrania. Siku ya kumi ni karibu na mwanzoni mwa mwezi wa kwanza katika kalenda za Magharibi.

mfalme wa Babeli ameizingira Yerusalimu

Jeshi la Babeli linarejewa kwa sababu ya kiongozi wake.

Ezekiel 24:3

jaza mifupa chini yake

Baadhi ya tamaduni huchoma mifupa kuichoma kwa sababu huungua mda mrefu kuliko kuni.

Ezekiel 24:6

chungu kinachopikwa

Yahwe anailinganisha Yerusalemu na chungu kinachopikwa.

kutu

ni kitu chekundu kilichotengenezwa juu ya chuma. Kutu hula chuma na mwishowe huiharibu chuma

Chukua

Yahwe hatoi hii amri kwa mtu maalumu, badala yake anaamuru baadhi picha ya mtu ambaye ni sehemu ya mfano.

Ezekiel 24:7

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa watu wa Yerusalemu.

yeye

Neno "yeye" linarejea kwa Yerusalemu, ambayo inawakilishwa na chungu kinachopikwa.

imeiweka juu ya jiwe laini

"ameweka damu juu ya mawe yaliyofunuliwa"

kuifunika kwa vumbi

"na kuifunika kwa vumbi"

Ezekiel 24:9

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kuilinganisha Yerusalemu na chungu kinachipikwa.

pia niataongeza chungu cha kuni

Inaonyesha kwamba nguzo ya mbao i chini ya chungu kunachopikwa, ambacho kinaiwakilisha Yerusalemu.

weka ... washa ... pika ... acha mifupa iteketee

Yahwe anato amri hii kufikirika watu ambao ni sehemu ya mfano.

acha mifupa iteketee

"choma mifupa"

Ezekiel 24:11

kuchoma

kuchoma uso wa kitu

kutu

Wakati kitu kinasababisha chuma kuvunjika vipande kwa kutu.

kula

"kuchomwa"

Amekuwa muoga

"Yerusalemu imechoka"

kazi na taabu

kazi ngumu

Ezekiel 24:13

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendlea kunena na Yerusalemu kwa kuilinganisha na chungu kilichopikwa.

Ezekiel 24:14

kazi zako, watakuhukumu

kile walichokifanya kinaonyesha wana hatia ya dhambi.

hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo

huu ni usemi wa Bwana Yahwe.

Ezekiel 24:15

neno la Yahwe likaja

"Yahwe akanena neno lake."

tamaa ya macho yako

Hii inarejea kwa mke wa Ezekieli. Yahwe anarejea kwa Ezekieli kwa sehemu ya mwili wake anatumi kumuona mke wake.

lakini hutakiwi kuomboleza wala kulia, na machozi yako hayatatoka

Haya maneno kimsingi yanamaanisha kitu kimoja na kusisitiza kwamba Ezekieli hatakiwi kumlilia mke wake anapokufa. "hutakiwi kuonyesha huzuni yako"

kilemba

kitambaa kirufu kilichotengezwa kwa ajili ya kufunga kwa kuzunguka kichwa.

makubadhi

viatu rahisi vinavyo valiwa kwenye miguu.

akini usivalishe shela nywele zako

Katika Israeli, wanaume walinyoa ndevu zao kuonyesha huzuni, kisha kufunika nyuso zao hata kwenye nywele zao. Yahwe alimwambia Ezekieli asiufunike nywele zake za mbele kuonyesha kwamba hakuwa amenyoa uso wake kuonyesha huzuni.

Ezekiel 24:19

Maelezo ya Jumla:

Watu wa Israeli wanamuuliza Ezekieli na Ezekieli anawaambia Yahwe alichowaambia.

Neno la Yahwe likaja

"Yahwe akanena neno lake."

kiburi cha nguvu zako

"kiburi katika kujenga kile ulicho kitengeneza"

tamaa ya macho yakow

"kutengeneza kile ulichokufurahisha kukitazama"

Ezekiel 24:22

utayeyuka

Hapa kupotea na kufa inazungumziwa kama kuyeyuka.

katika uovu wako

Hii inaonyesha kwamba Mungu hatasamehe dhambi za hawa watu. Ingawa, baadhi ya matoleo ya kisasa yanatafsiri "kwa sababu ya dhambi zako"

gugumia

sauti mtu afanyayo anapohitaji msaada, lakini maumivu au huzuni inakuwa kali sana kwamba hawawezi kuzungumza.

Ezekiel 24:25

mkimbizi

mtu aliyelazimishwa kuondoka kwenye nchi yao kwa sababu ya vita au janga jingine.

kinywa chako kitafunuliwa

"Yahwe atafunua kinywa chako" Hii inaelezea mtu kueleweshwa na uwezo wa kuzungumza kuhusu kitu.

utaongea-hutakuwa bubu tena

Haya maneno yote yanamaanisha watu wa Israeli watazungumza. Inasema tena kama hasi kusisitiza chanya.

itakuwa ishara

Hii inarejea kwa watu wa Israeli kama ishara kwa sababu watawasaidia wakimbizi kuelewa kwa nini Yerusalemu iliharibiwa.

Ezekiel 25

Ezekiel 25:1

neno la Yahwe likaja

"Yahwe akanena neno lake."

Mwanadamu

Tazama tafsiri yake katika 2:1.

weka uso wako juu ya

Tazama tafsiri yake katika 4:1.

watu wa Amoni

"uzao wa Amoni" au "wale waishio katika nchi ya Amoni"

na tabiri juu ya

Tazama tafsiri yake katika 4:6.

Ezekiel 25:3

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anamwambia Ezekieli kuwaeleza watu wa Amoni.

watu wa Amoni

uzao wa Amoni" au "wale waishio katika nchi ya Amoni

Sikia neno la Bwana Yahwe

"Sikiliza huu ujumbe kutoka kwa Bwana Yahwe"

umesema, "Anhe!

Neno "Enhe" ni sauti ambayo watu hufanya wakati wakiwa na furaha kuhusu jambo. Katika kesi hii watu walikuwa na furaha kwa sababu mambo mabaya yalitokea kwa watu wa Israeli na Yuda. "umecheka"

juu ya patakatifu pangu wakati palipokuwa pamehasiwa

"juu ya patakatifu pangu wakati adui alipo paasi." "wakati adui wa kijeshi alipohasi hekalu langu"

juu ya nchi ya Israeli wakati ilipokuwa ukiwa

"wakati nchi ya Israeli ilipokuwa katika uharibifu"

juu ya nyumba ya Yuda wakati walipoenda kwenye uhamisho

"wakati walipo watazama watu wa Yuda mbali na watumwa."

tazama!

"tazama!" au sikiliza!"

niakupatia watu katika mashariki kama milki yao

"nitalifanya jeshi kutoka nchi ambayo ni mashariki yako kuja na kukutawala"

Wataweka kambi juu yako na kuweka hema zao miongoni mwako

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya: "Wataweka hema na kuishi katika nchi yako."

watu wa Amoni shamba kwa ajili ya mifugo

Hapa "watu wa Amoni" inarejea kwa nchi ambayo ni mali ya watuwa Amoni.

Ezekiel 25:6

pamoja na dharau ndani yako dhidi ya nchi ya Israeli

"pamoja na chuki yote uliyoijaza mbele ya watu wanaoishi katika Israeli"

tazama!

"tazama!" au "sikiliza!"

nitakunyooshea mkono wangu

"nitakupiga kwa mkono wangu wenye nguvu" au nitakuadhibu"

na kukutoa kama mateka kwa mataifa

"na nitayafanya mataifa kuja na kuchukua kila kitu mbali nanyi"

nitakukatilia mbali kutoka watu ... kukufanya adhabu miongoni mwa mataifa.

Haya maneno kimsingi yanamaanisha jambo moja na kusisitiza Yahwe atawaangamiza kabisa watu wa Amoni ili kwamba wasiwe taifa tena.

utajua yakwamba mimi ni Yahwe

Tazama tafsiri yake katika 6:6.

Ezekiel 25:8

tazama!

"Ona!" au "sikia!"

ntafungua miinuko ya Moabu, kuanzia kwenye miji yake juu ya mpaka

"nitaifungua njia ya kwenda Moabu kwa kuiangamiza miji juu ya mpaka wake."

uzuri wa Beth Yeshimothi, Baal Meoni, na Kiriathaimu

"nitaanza na miji mikubwa ya Beth Yeshimothi, Baali Meoni, na Kiriathaimu."

kwa watu wa mashariki waliokuwa juu ya watu wa Amoni

"nitatuma jeshi lile lile kutoka mataifa katika mashariki aliyeiteka Amoni."

Nitawapatia kama milki ili kwamba watu wa Amoni hawatakumbukwa miongoni mwa mataifa

"nitayafanya majeshi kuishinda Amoni ili kwamba pasiwe na mtu hata wa kuwakumbuka."

watajua yakwamba mimi ni Yahwe

Tazama tafsiri yake katika 6:6.

Ezekiel 25:12

Nitaunyoosha mkono wangu juu ya Edomu

Tazama tafsiri yake katika 25:6.

kutoka Temani hata Dedani

Haya ni majiji mawili mkabala na Edomu. Hii inamaanisha kwamba Mungu ataiangamiza Edomu yote.

Wataanguka kwa upanga

Neno "anguka" inawakilisha kuuawa na "upanga" inarejea kwa vita. "Maadui zao watawaua kwa upanga wao"

Ezekiel 25:14

Nitaweka kisasi changu juu ya Edomu kwa mkono wa watu wangu Israeli

"nitawatumia watu wa Israeli kulipa kisasi juu ya watu wa Edom"

watafanya kwa Edomu kulingana na hasira yangu na ghadhabu yangu

"wataionyesha Edomu hasira yangu na ghadhabu"

hasira yangu na ghadhabu yangu

Neno "ghadhabu" kimsingi linamaanisha kitu kimoja na kuongeza neno "hasira." "hasira yangu ya ghadhabu"

watakijua kisasi changu

"watu wa Edomu watajua ya kuwa nimelipa kisasi juu yao"

hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo

"Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo" "Hivi ndivyo Bwana asemavyo itakuwa"

Ezekiel 25:15

Wafilisti wamelipiza kisasi pamoja na uovu na kutoka ndani yao wamejaribu kuiharibu Yuda tena na tena

"Kwa sababu Wafilisti waliwachukia watu katika Yuda na kujaribu kulipa kisasi juu yao na tena"

Tazama!

"Tazama!" au "Sikia!"

Nitanyoosha mkono wangu dhidi ya Wafilisti

"nitaurudisha mkono wangu wa uweza juu ya Wafilisti"

nitakatilia

"nitaangamiza"

Wakerethi

"Watu wa Kerethi." Hawa ni watu walioishi katika Filisti

watajua yakwamba mimi ni Yahwe

Tazama tafsiri yake katika 6:6.

Ezekiel 26

Ezekiel 26:1

katika mwaka wa kumi na moja

"katika mwaka wa kumi na moja ya uhamisho wa Mfalme Yehoyakini"

katika siku ya kwanza ya mwezi

Haijulikani ni mwezi gani wa kalenda ya Kiebrania Ezekieli alio umaanisha.

neno la Yahwe likaja

"Yahwe alinena neno lake."

Mwanadamu

Tazama tafsiri yake katika 2:1.

Tire alisema juu ya Yerusalemu

"watu wa Tire wamesema juu ya watu wa Yerusalemu."

Enhe!

"Ndiyo!" au "vizuri sana!"

Malango ya watu yamevunjwa

Watu wa Tire wanatumia haya maneno kurejea kwa Yerusalemu kana kwamba ilikuwa lango la mji ambalo wafanya biashara walipitia kutoka mataifa yaliyozunguka yalipitia.

Amenigeukia

Hapa neno "yeye" inarejea kwa neno "malango" ambayo "imegeuka" juu ya bawaba kufungua kwenda Tire.

nitajazwa

Hapa "kujazwa" inamaanisha kustawi. "nitafanikiwa"

ameharibiwa

"Yerusalemu imeharibiwa"

Ezekiel 26:3

Tazama!

"Tazama!" au "Sikia!"

nitayainua mataifa mengi juu yako kama bahari iiunuavyo mawimbi yake

Hapa neno "mataifa" inarejea kwa majeshi yao. "nitalikusanya jeshi kutoka mataifa ambayo ni makubwa na nguvu kama mawimbi katika bahari ya kitambaa."

minara

Mnara ni jengo refu lilitumika kuona kwa ajili maadui au kuficha ndani.

Nitafagia mavumbi yake mbali na kumfanya kama jiwe tupu

"nitalifanya jeshi kuuharibu mji kabisa, na hawatakuwa na kitu hapa hivyo utakuwa kama jiwe ambalo halina kitu juu yake."

Ezekiel 26:5

Atakuwa

Mara nyingi miji inarejewa kama "yeye." "Tire itakuwa" au "Itakuwa."

sehemu ya kuwekea nyavu kati ya bahari

Sehemu ya Tire ilikuwa kisiwa. "kisiwa kisichokuwa na kitu kilitumika kwa ajili kukaushia nyavu za samaki"

hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo

Tazama tafsiri yake katika 5:11.

pora

vitu ambavyo watu walivyovipoteza

atakuwa mateka kwa mataifa

"majeshi kutoka mataifa wataiba kila kitu kutoka Tire."

Binti zake walioko mashambani watachinjwa kwa panga

"Adui wa jeshi atawaua mabinti zake ambao wapo katika uwanda."

Binti zake waliopo katika uwanda

Wakati mwingine vijiji viliitwa mabinti vya miji iliyotawala juu yao. wasichana wa Tire waliokuwa wakifanya kazi katika mashamba.

watajua yakuwa mimi ni Yahwe

Tazama tafsiri yake katika 6:6

Ezekiel 26:7

Tazama!

"Ona!" "Sikia!"

namleta Nebukadreza

Mungu anamtumia Nebukadreza kuleta kuhusu mapenzi yake.

mfalme wa waflme

"mfalme mwenye nguvu zaidi"

watu wengi sana

Haya maelezo yansisitiza ukubwa wa jeshi la Nebukadneza.

Atawaua mabinti zako

Hapa neno "Yeye" linamrejea Nebukadreza ni mfano kwa jeshi.

Ezekiel 26:9

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa Tire.

Ataweka

Neno "yeye" inamrejea Nebukadneza, mfalme wa Babeli.

vyombo vya kubomolea

Tazama tafsiri yake katika 4:1.

vifaa vyake

"vifaa vyake vya vita"

Ezekiel 26:12

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendela kumpatia ezekieli ujumbe wake kwa Tire.

Ezekiel 26:15

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa Tire.

visiwa havitatetemeka ... kati yako

"Tetemeko la kisiwa ... kati yako."

Ezekiel 26:17

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa Tire.

Ezekiel 26:19

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa Tire.

kukufanya

Neno "wewe" linarejea kwa mji wa Tire.

Ezekiel 27

Ezekiel 27:1

neno la Yahwe likaja

"Yahwe akanena neno lake."

anayeishi kati ya malango ya bahari

"anayeishi kwenye malango ya bahari." "aishiye karibu na bandari ya bahari."

Ezekiel 27:4

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa Tire.

mipaka yako

"Mipaka ya himaya yako"

mlingoti

ni nguzo ndefu inayoshika matanga ya meli.

Ezekiel 27:6

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia ezekieli ujumbe wake kwa Tire.

makasia

vipande virefu vya mbao ambavyo watu hutumia kutengenezea boti kutembea

sitaha

ni sehemu za boti ambazo watu wanaweza kutembea juu yake

pembe

nyeupe, nzuri, na nyenzo ngumu ambayo imetengenezwa kutokana na meno ya wanyama.

tanga

vipande vya nguo vinavyoendesha meli wakati upepo uvumapojuu yao

Ezekiel 27:8

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia ezekieli ujumbe wake kwa Tire.

marubani

watu wanaoelekeza meli wapi iende

jaza mishono yako

"kukutengeneza nyufa"

maharia

watu wanaotanga meli katia bahari

Ezekiel 27:10

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa tire.

watu wa vita

"watu waliopigana katika vita vyako" au "kutumika kama wapiganaji wako"

walionyesha uzuri wako

"walikutoa uzuri wako!"

Ezekiel 27:12

Maelezo ya jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekeili ujumbe wake kwa Tire.

chuma

chuma kigumu kilichokuwa kizuri kwa kutengenezea silaha na kujengea vitu

bati

chuma kilicho bakia baada kusafisha dhahabu, fedha au chuma

risasi

ni chuma cha thamani ambacho ni kizito sana na kilaini kuliko vyuma vyote

Yavani

ni taifa katika ufunkwe wa magharibi mwa Asia ndogo.

Ezekiel 27:14

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia ezekieli ujumbe wake kwa Tire.

farasi dume

farasi dume mwenye nguvu

Bidhaa zilikuwa mkononi mwako

"Umemiliki mizigo."

Ezekiel 27:16

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendela kumpatiaEzekieli ujumbe wake kwa Tire.

zambarau

"nguo ya zambarau"

lulu

vipande vya kitambaa cheupe kigumu ambacho hutoka viumbe katika bahari

keki

"chakula kizuri kilicho tengenezwa kwa unga."

rubi

mawe mekundu ambayo ni ya thamani sana

lihamu

utomvu utokao kwenye mti

Ezekiel 27:19

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa Tiro.

mdalasini

aina ya kiungo kinachotoka kwenye gome la mti.

mchai chai

ni aina ya majani ambayo watu hutumia kama manukato na kwa ajili ya dawa.

blangeti la shogi

kipande cha nguo ambacho watu wameweka juu ya farasi chini ya shogi

Ezekiel 27:22

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia ezekieli ujumbe wake kwa Tire.

vito vya thamani

"mawe ya thamani"

Ezekiel 27:24

Maelezo ya Jumal:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa Tire.

mapambo ya joho ya nguo za urujuani pamoja na rangi

"majoho ya zambarau pamoja na rangi nyingine tofauti tofauti"

blangeti za zenye rangi tofauti tofauti, nakshiwa, na nguo zilizo sanifiwa vizuri

nguo zilizosanifiwa - "blangeti zenye rangi tofauti tofauti zilizokuwa zimebuniwa na kuvaliwa kwa hali ya juu"

katika moyo wa bahari

"katikati ya njia zote za biashara kwa ajili ya bahari ya biashara."

Ezekiel 27:26

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia ezekieli ujumbe wake kwa Tire.

Wapiga makasia wako walikuleta kwenye bahari kuu mno

"Watu wapigao kasia wamekuleta kutoka kwenye bahari"

katikati yao

"katikati ya bahari"

Ezekiel 27:28

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa tire.

watalia kwa sauti

"watapiga unyende kwa huzuni kubwa"

Ezekiel 27:31

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa Tire.

watanyoa vichwa vyao upaa

"watanyoa vichwa vyao hivyo hawatakuwa na nywele"

Ni nani aliye kama Tire

"Hakuna mji mwingine kama Tire."

ambaye sasa ameletwa kunyamazishwa

"nani ameangamizwa."

ufukwe

"juu ya nchi"

Ezekiel 27:34

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa Tire.

walikuogopa

"walishtuka na kuogopa kwa kile kilichotokea kwako"

kukuzomea

Kuzomea ni njia ya kuonyesha huzuni.

umekuwa tishio

"imekuwa tishio kwa watu kufikiria kuhusu wewe"

Ezekiel 28

Ezekiel 28:1

neno la Yahwe likaja

"Yahwe akanena neno alake."

katika moyo wa bahar

Tazama tafsiri yake katika 27:4.

umeufanya moyo wako kama moyo wa mungu

"unafikiri kwamba kumbukumbu wa mungu"

Ezekiel 28:4

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa mtawala wa Tire.

kwa hekima na ujuzi

"kwa hekima yako na uelewa wako"

na kujipatia

"na kujihifadhia"

hazina

mahali pa kuhifadhia vitu vya thamani na kuviweka salama

Ezekiel 28:6

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa mtawala wa Tire.

umetengeza moyo wako kama moyo wa mungu

Tazama ilivyo tafsiriwa katika 28:1, "umeufanya moyo wako kama moyo wa mungu.

uzuri wa hekima yako

"uzuri wa mji ambao ulioujenga kwa hekima yako."

Ezekiel 28:8

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea lumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa mtawala wa Tire.

Je! kweli utasema, "Mimi ni mungu"

"Hutatakiwa kutamani kusema, "mimi ni mungu."

nimesema hili-asema Bwana Yahwe

Tazama tafsiri yake katika 5:11.

Ezekiel 28:11

Neno la Yahwe la Yahwe

"Yahwe akanena neno lake."

inua maombolezo

"imba nyimbo ya msiba" au "imba wimbo wa kuomboleza"

Ulikuwa mfano wa ukamilifu

"Ulikuwa mkalifu."

umejaa hekima na ukamilifu wa hekima

"hekima kubwa na mwenye umbile zuri sana"

Kila jiwe la thamani lilikufunika

"ulivaa kila aina ya jiwe la thamani." Hii inaonyeshaalikuwa tajiri sana.

almasi, zabarajadi, shohamu,yaspi, yakuti samawi, zumaridi, baharamani, na dhahabwamba mfalme

Haya yote ni mawe ya thamani ya rangi tofauti tofauti.

Ezekiel 28:14

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa mfalme wa Tire.

mawe ya moto

"mawe ya moto."

kutoka siku ulipoumbwa

" tangu siku niliyokuumba."

Ezekiel 28:16

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa mfalme wa Tire.

mawe ya moto

Tazama tafsiri yake katika 28:14.

mbele

"mbele ya"

Ezekiel 28:18

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa mfalme wa Tire.

watakuwa watu wa kutisha, na hutakuwepo tena milele

Tazama tafsiri yake katika 27:34.

Ezekiel 28:20

neno la Yahwe likaja

"Yahwe akanena neno lake."

Mwanadamu

Tazama tafsiri yake katika 2:1.

weka uso wako juu ya

Tazama tafsiri yake katika 4:1.

tabiri juu ya

Tazama tafsiri yake katika 4:6.

Tazama!

"Ona!" au "Sikia!"

Ezekiel 28:23

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa Sidoni.

4Kisha hakutakuwa na mtemba uchomao na maumivu ya miba kwa ajili ya nyumba ya Israeli kutoka wale wote waliomzunguka wanaowadharau watu wake

"Hakutakuwa na watu mahali popote kuzunguka watu wa Israeli waliowajeruhi kama mitembe inayoparua na kuwaumiza kama miiba inayosababisha maumivu."

Ezekiel 28:25

kati yake

"katika nchi"

Ezekiel 29

Ezekiel 29:1

Katika mwaka wa kumi

"Katika mwaka uhamisho wa Mfalme Yehoyakini"

katika mwezi wa kumi katika siku ya kumi na mbili ya mwezi

"katika siku ya kumi na mbili ya mwezi wa kumi." Huu ni mwezi wa kumi wa kalenda ya Kiebrania. Siku ya kumi na mbili iliyo karibu na Mwezi wa kwanza katika kaelenda za Magharibi.

neno la Yahwe likaja

"Yahwe akanena neno lake." Tazama tafsiri yake katika 1:1.

joka kubwa

"dubwana kubwa liishilo katika maji." Yahwe anaanza kumlinganisha Farao na dubwana liishilo katika maji. Dubwana linafanana kama mambo.

Ezekiel 29:4

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa Faro, akimlinganisha na dubwana katika maji.

ndoana

vipande vikali au ubao ambao watu hutumia kukamatia samaki na wanya wengine katika maji

maganda

vipande vigumu vilivyo juu ya samaki, mambo na wanyama wengine

Ezekiel 29:6

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe kwa Farao.

wamekuwa mwanzi wa kutegemewa

Yahwe anawalinganisha watu wa Misri na Farao na mwanzi kwa sababu watu wa Israeli waliwategemea Wamisri kuwasaidia katika vita, lakini Wamisri hawakuwa imara kuwasaidia.

mwanzi

mmea ukuao karibu na maji na unafanana na majani marefu

shina

sehemu ya mwanzi ambayo ni ndefu kama fimbo nyembamba. Watu wanaweza kuzitumia kama fimbo.

watakapo kushika

Neno "wewe" linamreja Farao.

Ezekiel 29:8

Maelezo ya jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia ezekieli ujumbe wake kwa Faro.

Tazama!

"Ona!" au "Sikia!"

upanga juu yako

Neno "wewe" ni imoja wa mwanamke na inarejea kwa taifa la Misri.

juu yako

Neno "wewe" umoja wa mwanamume na inamrejea Farao.

kutoka Migdoli hata Sewene

"Katika Misri yote" au "kutoka mpaka wa kaskazini mwa Misri hata mpaka wa kusini mwa Misri."

Ezekiel 29:11

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa Farao.

hakuna mguu wa wanyama pori watakao upitia

"hakuna hata mnyama atatembea humo"

Ezekiel 29:13

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa Farao.

walikuwa wametawanyika

"nimewatawanya."

nitawarudisha wageni wa Misri

"kuwapatia Misri kile kilichokuwa kimepotea"

mkoa wa Pathrosi

sehemu ya kusini mwa Misri kati ya Delta na nchi ya Kushi. Hii pia inaitwa Misri juu.

Ezekiel 29:15

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa Farao.

Wamisri hawatakuwa sababu kwa ajili ya imani kwa ajili ya nyumba ya Israeli

"Taifa la Israeli halitaaminika kwa Wamisri"

walipogeukia Misri kwa ajili ya msaada

"Popote walipoenda hata Misri kwa ajili ya msaada"

Ezekiel 29:17

katika mwaka wa ishirini na saba

mwaka wa saba - "katika mwaka wa ishirini na saba ya uhamisho wa Mfalme Yehoyakini"

katika siku mwezi wa kwanza

"katika siku ya kwanza ya mwezi." Huu ni mwezi wa kwanza wa kalenda ya Kiebrania. Hii siku ya kwanza ipo karibu na mwanzoni mwa Mwezi wa nne.

neno la Yahwe likaja

"Yahwe akanena neno lake."

Mwanadamu

Tazama tafsiri yake katika 2:1.

Ezekiel 29:19

Tazama!

"Ona!" au "Sikia!"

Ezekiel 29:21

nitachipusha pembe kwa ajili ya nyumba ya Israeli

Hili neno linamaanisha "nitaifufua nguvu ya nyumba ya Israeli."

kati yao

"kwao"

Ezekiel 30

Ezekiel 30:1

Maelezo ya Jumla:

Ezekieli anaeleza kuhusu ujumbe ambao Yahwe alio mpatia.

Neno la Yahwe likja

"Yahwe akanena neno lake."

Mwanadamu

Tazama tafsiri yake katika sura ya 2:1.

Maombolezo

"Lia kwa huzuni" Hii amri ni kwa Misri na mataifa yanayoizunguka Misri.

Ole inakuja siku hiyo

"Hiyo siku itakuwa chungu sana" au "Mambo mabaya yatatokea siku hiyo"

Siku i karibu

Inaonyesha "hiyo siku" ilikuwa mda wakati watu wataomboleza.

Siku ikaribu kwa ajili ya Yahwe. Itakuwa

Hii inaonyesha kwamba siku hiyo, Yahwe atawaadhibu watu.

siku ya mawingu

"Itakuwa kama siku yenye giza la mawingu"

mda wa hukumu kwa ajili ya mataifa

"mda wakati mambo mabaya yatakapotokea kwa mataifa"

Ezekiel 30:4

Maelezo ya Jumla:

Haya ni maneno ya Yahwe kuhusu Misri

Kisha upanga utakuja juu ya Misri

Neno "upanga" hapa linarejea kwa vita au shambulizi. "Kutakuwa na vita juu ya Misri"

kutakuwa na maumivu makali katika Kushi

"Kushi itakuwa na huzuni sana" au "watu wa Kushi watakuwa na huzuni kubwa sana"

wakati wauaji wa watu watakapoanguka katika Misri

"wakati watu wa Misri watakapouawa" au "wakati watu wengi katika Misri watakapokufa katika vita."

wakati watakapochukua utajiri wake

"Washambuliaji watauchukua utajiri wa misri"

wakati msingi wake utakapoharibiwa

"Washambuliaji wataiharibu hata misingi ya majengo katika Misri"

Libya

Libya ni nchi ya magharibi mwa Misri.

Ludi

Hii ni kama inaurejea ufalme wa Ludi ambayo kwa sasa ni Uturuki. Ezekieli anaiita mkoa wa Ludi.

watu wa nyumba ya agano

"Wayahudi wanaoishi Misri"

wataanguka kwa upanga

"watakufa kwa mapambano" au "watakufa kwa upanga." Hii haimaanishi kwamba kila mtu atakufa, lakini kwamba watu wengi kutoka hizi nchi zote watakufa.

Ezekiel 30:6

Yahwe asema hivi

"Hivi ndivyo Yahwe asemavyo." Hii sentensi inatambulisha ambacho Yahwe atakisema.

Basi wale

"Katika njia hii" au "Katika namna hii, mataifa"

anayeisaidia Misri

"anayeisaidia misri"

wataanguka

"watakufa" au "wataharibiwa"

kiburi cha nguvu yake kitashushwa

"nguvu ya Misri, ambayo inaifanya ijiinue, itaondoshwa"

Kutoka Migdoli hata Sewene

Ezekieli ameipa miji majina upande wa mipaka ya Misri ili kuirejea Misri yote.

maaskari wao watanguka kwa upanga

Maaskari wa Misri watakufa kwa uapnga."

Wataogofya kati ya nchi zilizotupwa

"Maaskari wa washirika wa Misri wataogopwa wakati watakapoachwa wamezungukwa bila kitu lakini nchi tupu"

kati ya

"miongoni" au "kuzungukwa na"

miji yao itakuwa miongoni mwa miji yote iliyoangamizwa

"miji yao itazungukwa na miji iliyoharibiwa karibu na mataifa"

Ezekiel 30:8

Maelezo ya jumla:

Haya ni maneo ya Yahwe kuhusu Misri.

Kisha wata

"Kisha watu" au "Kisha Wamisri"

watajua kwamba mimi ndimi Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 6:6.

wakati nitakapoweka moto katika Misri

Moto unarwjea kwa moto ambao mara nyingi umetokea katika vita.

wasaidizi wake wote wameangamizwa

"nawaangamiza wote wanaohusiana na Misri" au "ninawavunja wote wanaoisaidia Misri."

wajumbe watatoka mbele yangu katika meli ili kuitia hofu Kushi

Wajumbe wataleta ujumbe wa kuingamiza Misri hata Kushi, nani atakuwa tishio kwa hii habari.

kuitia hofu Kushi

"ili kuitishia Kushi, ambaye sasa anajisikia yuko salama kutoka hatari"

kutakuwa na maumivu makali miongoni mwao katika siku ya kuangamizwa Misr

"watu wa Kushi pia watakuwa na maumivu makali nitakapoiadhibu Misri"

Inakuja

"ina" inarejea kwa "maumivu makali" au "huzuni kubwa" ambayo Kushi watakuwa nayo wakati watakapoadhibiwa pembeni ya Misri.

Ezekiel 30:10

Bwana Yahwe asema hivi

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:5.

Nitaufanya mwisho wa watu wa Misri

"nitafanya hivyo ili Misri isiwe na watu wengi."

kwa mkono wa Nebukadreza

Nebukadreza atakuwa yule ambaye aletaye hii hukumu.

Yeye pamoja na jeshi lake ... italetwa kuiharibu nchi

"nitamleta Nebukadreza na jeshi lake ... kuingamiza nchi"

Yeye pamoja na jeshi lake, hofu ya mataifa

Yahwe anamuita Nebukadrea "hofu ya mataifa" kwa sababu mataifa yote yana hofu kubwa ya jeshi lake.

kuiangamiza nchi

"hivyo wataiangamiza nchi." Yahwe atamleta Nebukadreza na watu wake ili waiangamize nchi.

watafuta panga zao juu ya Misri

"pigana juu ya Misri"

jaza nchi kwa maiti za watu

Hii ni kutia chumvi kuonyesha kwamba Wababeli watawaua Wamisri wengi sana.

Ezekiel 30:12

Maelezo ya Jumla:

Haya ni maneno ya Yahwe kuhusu Misri.

Nitaifanya mito kuwa nchi kavu

"Nitaikausha mito ya Misri"

nitaiuza nchi kwenye mkono wa watu waovu

Yahwe atawapatia Wababeli kutawala juu ya Misri kama mtu auzaye kitu kumpatia yule akununuaye kukitawala hicho kitu.

Nitaifanya nchi na viijazavyo ukiwa kwa mkono wa wageni

"Nitawafanya watu kutoka taifa jingine kuiharibu nchi na kila kitu ndani yake"

viijazavyo

"kila kitu katika nchi"

Ezekiel 30:13

Bwana Yahwe asema hivi

Tazama tafsri yake katika sura ya 5:5.

nitaleta mwisho wa sanamu za ubatili

"angamiza sanamu zisizo na maana"

Memfizi

Memfizi ulikuwa mji muhimu sana katika Misri. Ulikuwa karibu na Kairo ya mpya.

mwana mfalme katika nchi ya Misri

"mtawala muhimu katika nchi ya Misri"

nitaweka hofu katika nchi ya Misri

"nitawafanya watu wa Misri kuogopa sana"

Pathrosi

Huu ulikuwa mkoa katika kusini mwa Misri.

kuweka moto katika Soani,

"nitaichoma Soani kwa moto"

Soani

Soani ulikuwa mji mwingine muhimu katika Misri.

Thebesi

Huu ulikuwa mji mkuu wa kusini mwa Misri.

Ezekiel 30:15

Maelezo ya Jumla:

Haya ni maneno ya Yahwe kuhusu Misri.

Kwa kuwa nitamwaga ghadhabu yangu juu Sini

"Kwa kuwa nitatenda hasira yangu juu ya Sini" au "Kwa sababu nina hsira sana, nitaiadhibu Sini mmoja mmoja"

Sini

Huu ulikuwa mji wa muhimu kaskazini mwa Misri.

kuwakatilia mbali kundi la Tebesi

"kuua hesabu kubwa ya watu katika Tebesi"

Tebesi

Tazama tafsiri yake katika sura ya 30:13.

Kisha nitaweka moto katika Misri

"nitaichoma Misri kwa moto"

Tebesi itavunjwa

"Tebesi itaangamizwa."

Kisha niweka moto katika Misri

"nitaichoma Misri kwa moto"

itakuwa katika dhiki kuu

"itakuwa katika maumivu makali"

Ezekiel 30:17

Maelezo ya Jumla:

Haya ni maneno ya Yahwe kuhusu Misri.

Heliopolisi na Pi-besethi

Hii ilikuwa miji katika upande wa kaskazini mwa Misri.

ataanguka kwa upanga

Neno "upanga" limetumika kurejea kwa mapambano au vita" au "watakufa kwa upanga."

miji yao itakwenda kwenye utumwa

"watu wa miji yao watakuwa mateka"

Tapanesi

Huu ulikuwa mji wa muhimu katika kaskazini mwa Misri.

Ezekiel 30:20

Kisha ikawa

Hili neno limetumika hapa kuonyesha mwanzoni mwa shemu ya kwanza ya hadithi.

katika mwaka wa kumi na moja

Tazama tafsiri yake katika sura ya 26:1.

katika mwezi wa kwanza, siku ya saba ya mwezi

"katika siku ya saba ya mwezi." Hii ni siku ya kwanza ya mwezi ya kalenda ya Kiebrania. Siku ya saba ni karibu na mwanzoni mwa mwzi wa Nne katika kalenda za Magharibi.

neno la Yahwe likaja

Yahwe akanena neno lake."

Mwanadamu

Tazama tafsiri yake katika sura ya 2:1.

vunja mkono wa Farao

Hapa "mkono" unawakilisha uweza wa mfalme.

Tazama!

Neno "Tazama" Hapa linatuweka macho kwa habari inayoshangaza kwa kile kifuatacho.

Haukufungwa, au kufungwa kwa kitambaa cha bendeji

"Mkono wake haujafungwa na hauna dawa ili uweze kupona"

bendeji

kipande laini ambacho watu huweka juu ya vidonda ili wapone

hivyo basi uweze kuwa imara kushika upanga

Hapa "upanga" unawakilisha uweza wa mfalme katika vita. "hivyo mkono wake hautakuwa hodari kutumia upanga"

Ezekiel 30:22

Bwana Yahwe asema hivi

tazama tafsiri yake katika sura ya 3:10.

wote yule aliye hodari na yule aliyevunjika

"wote mkono ambao ni mzima na mkono ambao umevunjika tayari"

nitaitawanya Misri miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbali mbali

Tazama tafsiri yake katika sura ya 20:23.

nchi

"nchi"

Nitaunyoosha mikono kwa mfalme wa Babeli

"nitaifanya mikono ya mfalme wa Babeli kuwa imara"

Atagugumia mbele ya mfalme wa Babeli

Wakati mfalme wa Babeli atakapokuja kuiteka Misri, Farao atagugumia.

gugumia

"Gugumia ni sauti kubwa ambayo watu hufanya wakati wanapokuwa na maumivu au kufa.

kwa mgumio wa mtu anayekufa

"kama mtu anayekufa agumiavyo" au "kama mtu anayekufa"

Ezekiel 30:25

5Kwa kuwa nitainyoosha mikono ya mfalme wa Babeli

"nitaufanya mikono imara ya mfalme wa Babeli."

wakati mkono wa Farao utakapoanguka

"lakini Farao hataweza kutumia mikono yake" au "mikono ya Farao itakuwa dhaifu kwamba hataweza kuitumia"

Kisha wata

Neno "wao" "Wamisri" au "watu wote wasikiao kile Yahwe alichokifanya."

jua kwamba mimi ndimi Yahwe

tazama tafsiri yake katika sura ya 6:6.

kwa kuwa ataishambulia nchi ya Misri kwa huo

"na mfalme wa Babeli ataishambulia nchi ya Misri pamoja na upanga"

nitaitawanya miongoni mwa mataifa na kuyatawanya kwenye nchi tofauti tofauti

Tazama tafsiri yake katika sura ya 20:23.

Ezekiel 31

Ezekiel 31:1

ikawa

Hili neno limetumika hapa kuonyesha mwanza wa sehemu nyingine ya hadithi.

katika mwaka wa kumi na moja

Tazama tafsiri yake katika sura ya 26:1.

katika tatu ya mwezi, siku ya tatu ya mwezi

"katika siku ya kwanza ya mwezi wa tatu."

neno la Yahwe likaja

"Yahwe akanena neno lake."

mwanadamu

Tazama tafsiri yake katika sura ya 2:1.

Katika ukuu wako, wewe ni kama nani?

"Ni nani aliye mkuu kama wewe?" Yahwe anatumia hili swali kutambulisha mada mpya. Farao alifikiri kwamba taifa lake lilikuwa kubwa zaidi, lakini Mungu anataka kuzungumzia taifa jingine.

Ezekiel 31:3

Maelezo ya Jumla:

Haya ni maneno ya Mungu kwa Farao kuhusu Ashuru. Mungu anatoa ujumbe wake katika mfumo wa fumbo kuhusu mti mkubwa wa mkangazi.

Tazama!

"Tazama!" au "Sikiliza!"

kivuli kwenye msitu

"inayo andaa kivuli kwa ajili ya miti mingine katika msitu."

na mrefu katika kimo,

"ndefu sana"

Urefu wa mti wake ulikuwa juu ya mawingu

"Urefu wa mti ulikuwa katika mawingu"

Maji mengi yaliufanya kuwa mrefu

"Kwa sababu mkangazi ulikuwa na maji mengi, ulirefuka sana"

vilindi vya maji yaliufanya mkubwa

"kilindi cha maji katika aridhi uliufanya mkangazi kuwa mkubwa sana"

mifereji yake ilitoa kuelekea kwenye miti yote katika shamba

"na mifereji ilitoa kutoka kwenye mito kwenda kwenye miti yote ya shamba."

Ezekiel 31:5

Maelezo ya Jumla:

Fumbo la Yahwe kuhusu mwerezi linaendelea.

Kimo chake kikubwa kilikuwa zaidi kuliko miti mingine yote katika shamba

"Mwerezi ulikuwa mrefu kuliko miti mingine yote ya shambani"

matawi yake yakawa mengi

"ulimea matawi mengi sana"

kwa sababu ya maji mengi ilimea

"kwa sababu ulikuwa na maji mengi"

Kila ndege wa mbinguni alitengeza kiota kwenye matawi yake

"Iina zote za ndege warukao angani walitengeza viota katika matawi yake"

wakati kila kiumbe hai cha shambani kilizaa mtoto chini ya tawi

"na viumbe vyote viishivyo katika shamba walizaa chini yamatawi ya mwerezi"

Mataifa mengi yote yaliishi chini ya kivuli chake

"mataifa yote yenye nguvu yaliishi katikakivuli chake"

ulikuwa uzuri katika ukuu wake na kimo cha matawi yake

"Ulikuwa mzuri kwa sababu ulikuwa mkubwa na matawi yake yalikuwa marefu sana"

Ezekiel 31:8

Maelezo ya Jumla:

Fumbo la Yahwe kuhusu mkangazi linaendelea

Mikangazi katika bustani ya Mungu haiwezi kuwa sawa

"Mwerezi katika bustani haukuwa mkubwa kama huo mti."

bustani ya Mungu

Hii ni njia nyingine ya kurejea bustani ya Edeni."

Hakuna miongoni mwa miti ya mivinje iliyofanana matawi yake

Yahwe alikuwa akinganisha kulikuwa na matawi mangapi.

miti ya mivinje

Miti ya mivinje ina matawi mengi sana. Yanaweza kurefuka sana.

miamori haikuweza kuwa sawa na majani yake

Ilikuwa inamwonyesha Yahwe kulinganisha matawi marefu ya mti wa mwerezi pamoja na matawi marefu ya mwamori.

mierezi

Mierezi ni mirefu, miti yenye majani na matawi imara. Inafanana na mikuyu.

ulikuwa kama huo katika uzuri wake

"ulikuwa mzuri kama mti wa mwerezi"

Nimeufanya kuwa mzuri pamoja na matawi yake

"Nimeufanya mwerezi kuwa mzurri kwa kuupatia matawi marefu."

aliuonea wivu

"alikuwa na wivu wa mti wa mkangazi"

Ezekiel 31:10

Maelezo ya Jumla:

Fumbo la Yahwe kuhusu mkangazi linaendelea

weka urefu wake

Hili fungu linaendelea kumrejea mfalme wa Ashuru, ambaye aliwakilishwa na mkangaze.

Nimeuweka kwenye mikono ya yeye mwenye uweza wa mataifa

"nimemuweka kwenye nguvu ya taifa imara zaidi." Neno "mkono" linawakilisha utawala.

Nimeufukuza

"nimeupeleka mkangazi mbali kutoka nchi ya mkangazi kwa sababu mkangazi ulikuwa dhaifu"

Ezekiel 31:12

Maelezo ya Jumla:

Fumbo la Yahwe kuhusu mkangazi linaendelea.

waliokuwa wakiogofya mataifa yote

"walio wafanya mataifa yote kuogopa"

kuukatilia mbali

"kuukatilia mkangazi chini"

matawi yake yameanguka

"wageni walivunja matawi ya mkangazi"

matawi

Ni matawi marefu yameayo kwenye miti.

wakatoka nje kutoka chini ya kivuli

"acha kivuli cha mkangazi"

Ezekiel 31:13

Maelezo ya Jumla:

fumbo la Yahwe kuhusu mkangazi linaendelea.

Ndege wote wa angani

"Ndege wote warukao angani"

wakapumzika juu ya shina lake

"wakaishi juu ya mkangazi uliosalia"

shina

ni sehemu nene sana ya mti ambao hutoka aridhini na kuzishikilia sehemu nyingine za mtu.

wanyama wa shambani atakuja kwenye matawi yake

"wanyama pori waliishi katika matawi ya mkangazi"

mwagilia maji

"miti ipatayo maji mengi"

hakuna mti mwingine utakayomea karibu na maji itakayofikia kwenye huo urefu

"na hakuna miti mingine ambayo itapata maji mengi itarefuka huo urefu ttena"

chini kabisa hata kwenye nchi

"na nimeufanya ili waende chini ya aridhi."

katikati ya watu wa mwanadamu aliyeenda chini hata kwenye shimo

"kuwa na hao watu waliokufa na kwenda chini kwenye kaburi"

Ezekiel 31:15

Maelezo ya Jumla:

fumbo la Yahwe kuhusu mkangazi linaendelea.

Katika siku ambayo mkangazi utakapo shuka kwenda Sheoli

Neno "kwenda chini hata Sheoli" maana yake "kufa." "Katika siku ambayo mkangazi utakapokufa"

nilileta maombolezo kwenye dunia

"nimeifanya nchi kuomboleza."

Nilifunika vilindi vya maji juu yake

Neno "funika" ni kama linarejea juu ya mavazi kwa ajili ya kuomboleza. "nimefanya maji kutoka chemichemi kuomboleza kwa ajili ya mkangazi"

nikayarudisha maji ya bahari

"nilitunza maji katika bahari kutoka kumwagilia nchi"

Nilizuia maji makuu

"Nilifanya hivyo ili kusiwe na maji mengi tena"

nikaleta maombolezo hata Lebanoni kwa ajili yake.

"na nikaitengeneza Lebanoni kwa ajili ya mkangazi"

Ezekiel 31:16

Maelezo ya Jumla:

fumbo la Yahwe kuhusu mkangazi linaendelea

wakati nitakapo mtupa chini hata Sheoli

"wakati nitakapomtupa chini hata Sheoli. "Hili neno linamaanisha, "wakati nitakapouua mkangazi."

pamoja na wote walioenda chini kwenye shimo

"pamoja na kila mmoja aliyekuwa amekufa na kwenda kwenye nchi"

sehemu za chini kabisa za nchi

"zilikuwa zimeenda chini tayari kwenda chini ya aridhi"

imechaguliwa na miti iliyokuwa bora ya Lenanoni; miti iliyokunywa maji.

"miti bora ambayo kila mmoja atataka, miti ambayo ina maji mengi" "Hii ni miti ya Edeni ambayo ilikuwa katika sehemu ya mwisho ya ardhi.

chaguliwa

"Hiki ni kitu ambacho kila mtu atakitaka kwa sababu ni chema sana.

Ezekiel 31:17

Maelezo ya Jumla:

fumbo la Yahwe kuhusu mkangazi linaendelea.

walishuka chini pamoja nayo hata Sheoli

"Hiyo miti ya Lebanoni pia imekufa na kushuka chini hata Sheoli pamoja na mkangazi"

walikuwa wameuawa kwa upanga

"ambao maadui waliuawa kwa upanga" au "waliokufa katika mapigano"

Hili lilikuwa jeshi lake imara

"Hii miti ya Lebanoni ilikuwa jeshi lake imara." Neno "jeshi imara" maana yake "nguvu."

8Umefanana na nani hivi katika utukufu na ukuu kati ya mti wa Edeni?

Mungu anamuuliza Farao jili swali kumwonyesha kwamba fumbo linatumika kwake na nchi yake.

Kwa kuwa utashushwa chini

"Kwa kuwa nitakusha chini"

pamoja na miti ya Edeni

"kama miti mingine ya Edeni"

hata sehemu za mwisho za nchi

"hata sehemu ya chini katika aridhi"

miongoni mwa wasiotahiriwa

"utakuwa wapi na watu ambao hawajatahiriwa"

hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:11.

Ezekiel 32

Ezekiel 32:1

Kisha ikatokea

hili neno limetumika hapa kuonyesha mwanzao wa sehemu mpya wa hadithi.

katika mwezi wa kumi na mbili ... katika siku ya kwanza ya mwezi

Hii ni siku ya kumi na mbili na mwezi wa kalenda ya Kiebrania. Siku ya kwanza i karibu na mwishoni mwa Mwezi wa pili.

ya mwaka wa kumi na mbili

"ya mwaka wa kumi na mbili ya uhamisho wa Mfalme wa Yehoyakini"

neno la Yahwe likaja

"Yahwe akanena neno lake."

Mwanadamu

Tazama tafsiri yake katika sura ya 2:1.

Wewe ni kama mwana simba ... kama dubwana katika bahari

"Alifikiri alikuwa kama simba, lakini alikuwa kama jitu la kutisha kabisa.

kama mwana simba miongoni mwa mataifa

Misri ilikuwa imara kuliko mataifa mengine, kama simba ambao ni shupavu kuliko wanyama wengine.

Ezekiel 32:3

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na Farao na kumfananisha na jitu la kutisha liishilo katika maji.

Bwana Yahwe asema hivi

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:5.

Basi nitautandaza wavu wangu juu yako katika kusanyiko la watu wengi

"Basi nitawakusanya watu wengi na kutupa wavu wangu juu yako."

watawainua juu katika wavu wangu

"kutumia wavu wangu, watu watakuvuta kutokakwenye maji"

Nitakuacha katika nchi

"Nitakuacha bila msaada katika nchi." Jitu la kutisha lililokuwa linatisha wakati lilipokuwa ndani ya maji haliwezi kufanya chochote wakati likiachwa juu ya nchi kavu.

ndege wote wa angani

"ndege wote warukao katika anga"

njaa ya wanyama wote waishio juu ya nchi watashibishwa na wewe

"nitawaacha wanyama wote wa nchi wataula mwili wako hadi njaa iwaishe"

Ezekiel 32:5

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na Farao na kumlinganisha na dubwana liishilo ndani ya maji.

funza wako waliokufa

"mwili wako uliokufa"

Kisha nitamwaga damu yako juu ya milima

"nitaifurika nchi damu kwa damu moja kwa moja hata kwenye milima."

vitanda vya kijito vitajazwa kwa damu yako

"nitaijaza mito kwa damu yako"

Ezekiel 32:7

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumwambia Farao atafanya nini juu ya Misri.

Kisha wakati nitakapo izimisha taa yako

"Yahwe analinganisha jinsi atakavyo muangamiza Farao kwa jinsi atakavyoweka moto wa taa. "Wakati nitakapokuharibu"

nitazifunika mbingu

Yahwe ataifunika anga ili kwamba watu wa nchi hawawezi kuona mwanga wa nyota, jua na mwezi.

giza na nyota zake

"nitazifanya nyota giza." Hakutakuwa na nuru.

nitaweka giza juu ya nchi

"nitalifanya giza katika nchi yako"

hili ni tangazo la Bwana Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:11.

Ezekiel 32:9

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na Farao.

nitaitisha mioyo ya watu wengi

"nitaifanya mioyo ya watu wengi kuogopa"

katika nchi ambao huwajui

Jinsi ambavyo Yahwe atakavyoiangamiza Misri itaogofya hata watu katika nchi ambayo Farao hajawahi kuifahamu ataifahamu.

wakati nitakapoleta kuhusu uvunjifu miongoni mwa mataifa

"wakati mataifa watakaposikia kuhusu jinsi nitakavyokuangamiza"

Nitawashangaza watu wengi kuhusiana na wewe

"nitawafanya watu wengi kuogopa kwa sababu ya kile kilichotokea kwako"

Ezekiel 32:11

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na Farao.

Upanga wa mfalme wa Babeli utakuja juu yako

Neno "upanga" inarejea hapa kwa jeshi. "Jeshi la mfalme wa Babeli watakushambulia"

Nitawafanya watu wako kuanguka kwa panga za mashujaa

"nitawafanya watu wako kuanguka kwa sababu ya panga za watu wenye uweza"

kila shujaa ni tishio la mataifa

"Kila shujaa ataogofya mataifa"

na kuangamiza watu wake wote

"na kuua hesabu kubwa ya watu waishio katika Misri"

Ezekiel 32:13

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendela kunena

mifugo yote

Mifugo ni wanyama ambao watu wanao kwa ajili ya kula na kwa sababu nyingine. Ng'ombe, kondoo, na mbuzi vyote ni mifugo.

karibu na maji mengi

"kutoka mahali ambapo kuna maji mengi"

mguu wa mtu

"miguu ya watu"

Kisha nitayafanya maji kuwa masafi

"nitayafanya maji kuwa masafi."

fanya mito yao kukimbia kama mafuta

Mafuta hutiririka pole pole na laini.

hili ndilo tangazo la Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:11.

Ezekiel 32:15

Maelezo ya jumla:

Yahwe anaendelea kunena.

nchi iliyojaa

"nchi iliyojaa viumbe hai"

wakati nitakapo washambulia wenyeji wote

"wakati nitakapowaangamiza waishio huko"

jua ya kwamba mimi ndimi Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura yha 6:6.

Kutakuwa na maombolezo

"Huu ni wimbo wa kuomboleza ambao watu wataimba"

binti za mataifa

"wanawake wa mataifa yote"

wataomboleza juu yake

Neno "yeye"linarejea kwa nchi ya Misri.

hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:11.

Ezekiel 32:17

Kisha ikawa

Hili nenao limetumika kuonyesha mwanzoni mwa ujumbe.

katika mwaka wa kumi na mbili

"Hii ilitokea katika mwaka wa kumi na mbili baada ya Wababeli kuwachukua Waisraeli kwenda Babeli.

neno la Yahwe likaja

"Yahwe akanena neno lake."

Mwanadamu

Tazama tafsiri yake katika sura ya 2:1.

omboleza kwa ajili ya watumishi wa Misri

"lia kwa sauti kwa ajili ya jeshi la Misri"

walete chini-yeye na binti za mataifa mashuhuri

"itupe Misri chini na binti za mataifa mashuhuri chini"

binti za mataifa mashuhuri

"watu wa mataifa yenye nguvu"

chini ya nchi

"sehemu chini ya ardhi."

pamoja na wale walioshuka chini kwenye shimo

"pamoja na kila mmoja yeyote aliyekuwa amekufa na kwenda aridhini"

shimo

"shimo" inarejea kwa kaburi. Ni shimo katika aridhi ambayo watu huenda baada ya kufa.

Ezekiel 32:19

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na Ezekieli

Waulize

"Waulize Misri na jeshi lake"

Nenda chini

Inaonyesha kwamba wanaenda chini hata Sheoli.

Wao

"Misri na jeshi lake"

wataanguka

"watakufa"

waliokuwa wameuawa kwa upanga

"ambao walikufa katika mapigano"

Misri amepatiwa upanga

"Maadui wataishambulia Misri"

maadui zake watamkamata na watumishi wake."

watumishi wake

kuhusu Misri na washirika wake

"kuhusu Misri na wale waliojiunga nao"

Ezekiel 32:22

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na Ezekieli kuhusu mataifa katika Sheoli.

Ashuru yupo huko pamoja na kusanyiko lake

"Watu wa Ashuru na jeshi lake lote wote wapo katika Sheoli"

wote waliuawa kwa upanga

"wote waliuawa kwa upanga" au "wote waliuawa katika mapigani"

yamewekwa katika maficho ya shimo

"yamewekwa katika sehemu ya chini kabisa ya shimo"

wote waliokuwa wameuawa, walioanguka kwa upanga

"wote ambao ni maadui waliuawa kwa upanga"

wale walioleta hofu juu ya nchi ya walio hai

"wale walisababisha watu katika nchi ya uhai kuogopa sana"

Ezekiel 32:24

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na Ezekieli kuhusu mataifa katika Sheole.

Elamu yupo huko

Hapa "Elamu" linarejea kwa watu wa hiyo nchi. "Watu wa Elamu pia wapo huko katika Sheoli"

watumishi wake

watu wake wengi au jeshi lake.

Makaburi yake yamemzunguka

Tazama tafsiri yake katika sura ya 32:22.

wote waliuawa

"Hapa maadui waliwaua wote"

Wale walioanguka kwa upanga

"walio anguka kwa upanga" katika 32:22.

waliokwenda chini wasiotahiriwa

"ambao walikuwa hawajatahiriwa wakati waliposhuka chini"

sehemu ya chini kabisa ya nchi

"sehemu za chini kabisa katika aridhi"

aliwaleta mashujaa wao juu ya nchi ya walio hai

Tazama tafsiri yake katika sura ya 32:22.

Wameweka vitu vya kitandani kwa ajili ya Elamu na watumishi wake

"Walimpatia Elamu vitanda na watumishi wake wote."

katikati ya wachinjaji

"pamoja na watu wote waliokuwa wameuawa."

Wote hawajatahiriwa

Wamisri waliwachukia watu ambao walikuwa wametahiriwa.

Elamu yu miongoni mwa wale waliokuwa wameuawa

"Maiti zilimpatia Elamu mahali kulala miongoni mwao wenyewe"

Ezekiel 32:26

Sentensi Unganishi

Yahwe anaendelea kunena na Ezekieli kuhusu mataifa katika Sheoli.

watumishi wao wote

"jeshi lao lote" au "watu wao wote."

Makaburi yao yamewazunguka

Tazama tafsiri yake katika sura ya 32:22, "kaburi lake limemzunguka."

Wote ... nchi ya uzima

Tazama tafsiri yake katika sura ya 32:24.

kinga yao imewekwa juu ya mifupa yao

Kutompenda mwingine asiyetahiriwa, Meshaki na watu wa Tubali walipewa mazishi yanayofaa.

Kwa kuwa walikuwa tishio kwa mashujaa katika nchi ya walio hai

"kwa sababu, wakati wakiwa bado hai, waliwafanya mashujaa kuogopa sana"

Ezekiel 32:28

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena.

utaangamizwa

"nitakuangamiza."

kati yao wasiotahiriwa

"karibu na watu wasiotahiriwa"

wale waliouawa kwa upanga

Tazama tafsiri yake katika sura ya 32:24.

Edomu yuko huko na wafalme na viongozi wake wote

"Edomu yupo katika Sheoli pamoja na wafalme na viongozi wake wote."

Walikuwa na nguvu

"Walikuwa na nguvu nyingi"

Ezekiel 32:30

Mwana mfalme wa kaskazini

"Wana mfalme waliotawala mataifa katika kaskazini"

wapo huko

"wapo katika Sheoli"

kwenda chini

"kwenda chini hata Sheole"

pamoja na maiti

"pamoja na wale waliokuwa wameuawa"

ambao waliokuwa wameuawa kwa upanga

"waliokuwa wameuawa kwa upanga"

Wamebeba aibu yao wenyewe, pamoja nao waendao kwenye shimo

"wamebeba aibu yao wenyewe, pamoja na wale wanaokwenda chini"

Ezekiel 32:31

Farao ataona

"Farao ataona maiti zote kutoka mataifa mengine."

na kupata faraja kuhusu watumishi wake

Inaonyesha kwamba Farao atafarijiwa kwa sababu maadui wa wafalme wengine wakubwa wamekufa pia.

ambao waliuawa kwa upanga

Tazama tafsiri yake katika sura ya 31:17.

hili ndilo tangazo la Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:11.

Natamuweka kama utiisho katika nchi ya walio hai

"Wakati Farao alipokuwa bado yupo hai, nilimruhusu kuwaogofya watu"

atakuwa amelala chini katikati yao wasiotahiriwa

Hapa "lala chini" inarejea kwa mwili wake kuwekwa katika kaburi wakati atakapokufa.

Ezekiel 33

Ezekiel 33:1

neno la Yahwe likaja

"Yahwe akanena neno lake."

Mwanadamu

Tazama tafsiri yake katika sura ya 2:1.

upanga juu ya nchi

Neno "upanga" linarejea kwa adui wa jeshi lishambulialo.

kumfanya mlinzi

"kumteua kama mlinzi"

usitilie manani

"puuza onyo"

damu ya kila mmoja iko juu ya kichwa chake mwenyewe

"ni kosa lao wenye kama wakifa"

Ezekiel 33:5

Maelezo ya jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa Waisraeli.

damu yake i juu yake

"itakuwa ni kosa lake mwenyewe kwamba amekufa"

okoa maisha yake mwenyewe

"atajiokoa mwenyewe kutoka kifo"

upanga kama ujavyo

Neno "upanga" inarejea kwa adui wa jeshi.

upanga ujao na kuchukua uhai wa mtu

"upanga ujao kumuua yeyote"

mtu akafa kwenye dhambi yake mwenyewe

"mtu atakufa kwa sababu ya dhambi yake mwenyewe"

Ezekiel 33:7

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na Ezekieli.

nyumba ya Israeli

Tazama tafsiri yake katika sura ya 3:1.

kutoka kwenye kinywa changu

"kutoka kwangu."

waonye badala yangu

"waonye kama muwakilishi wangu"

usitangaze hivi

"usiseme hivi"

kuhusu njia yake

"jinsi anavyotenda"

atakufa katika dhambi yake

Hii inaonyesha kwamba Mungu atasamehe dhambi za huyu mtu.

taka damu yake kutoka mkono wake

Tazama jinsi ilivyo tafsiriwa katika sura ya 3:16.

asipogeuka kutoka njia yake

"hataacha kutenda njia yake mbaya" au "hataacha kufanya mambo yake mabaya"

wewe mwenyewe utakuwa umeokoa maisha yako

"utajitunza mwenyewe hai"

Ezekiel 33:10

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa Wasraeli.

nyumba ya Israeli

Tazama jinsi ilivyo tafsiriwa katika sura ya 3:1.

Mnasema hivi

"Hivi ndivyo ulivyosema"

Makosa yetu na dhambi zetu

wanajisikia haitia kwa makosa yao na dhambi

na tunadhoofika kwa ajili yao

Hili neno linalinganisha jinsi dhambi inavyo muharibu mtu.

kati yao

Hii inamaanisha watu wanajua Mungu hatawasamehe.

Nitaishije?

Watu huuliza hili swali kusisitiza kwamba hawana tumaini la kuishi.

Kama niishivyo

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:11.

hili ndilo tangazo la Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:11.

kama mwovu akitubu kutoka njia yake?

"kama mtu muovu akiacha kufanya mambo mabaya"

kwa nini mnataka kufa

Yahwe anatumia hili swali kusisitiza kwamba hataki watu wa Israeli kufa.

Ezekiel 33:12

Maelezo ya Jumla:

yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa Israeli.

Haki ya mwenye haki haitamwokoa kama akikosa!

"Kama watu wenye haki wakianza kuasi, ukweli ni kwamba walikuwa wenye haki kabla hawatawaokoa"

kama akiamini katika haki yake

"kama akitegemea juu ya haki yake." Mtu anafikiri kwamba kwa sababu alikuwa na haki Yahwe hatamwadhibu, hata kama akiasi.

fanya isiyo haki

"fanya yaliyo maovu"

kwa ajili ya uovu alioufanya

kwa sababu ya mambo maovu aliyoyafanya.

Ezekiel 33:14

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia ezekieli ujumbe wake kwa Waisraeli.

kama akirudisha dhamana

"kama akirudisha dhamana"

dhamana

kitu ambacho mtu huacha kwa mtu mwingine kuonyesha kwamba atatunza ahadi yake kurudisha kile alichokiazima.

akirudisha kwa kile alichokipoteza

"rudisha kile alichokipoteza"

tembea katika maagizo yatoayo uzima

"kuishi kulinagana na sheria zitoazo uzima"

Dhambi alizozifanya hazitakumbukwa kwa ajili yake

"sitashikilia dhambi yake yoyote juu yake."

Ezekiel 33:17

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa Waisraeli.

watu wako

Hawa ni watu wa Israeli. Neno "wako" linamrejea Ezekieli.

lakini i kwenye njia zako

Neno "yako" linawarejea wana wa Israeli. "lakini ni njia zenu."

kufa katika hiyo

"kufa kwa sababu ya dhambi"

geuka kutoka uovu wake

"acha kufanya mambo maovu"

kwa sababu ya hayo mambo

"kwa sababu hufanya kilicho haki na haki"

enyi watu

Hawa ni watu wa Israeli.

Ezekiel 33:21

katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kumi

Huu ni mwezi wa kumi wa kalenda ya Kiebrania. Siku ya kumi na tano ni karibu na mwanzoni mwa Mwezi wa kwanza katika kalenda za Magahribi.

mateka wetu

Hapa "wetu" inarejea kwa Ezekieli na Waisraeli ambao walikuwa katika Babeli tangu wakati Wababeli walipomlazimisha Mfalme Yehoyakini kuondoka Yerusalemu.

mtu mmoja akatoroka kutoka Yerusalemuna

"mtu mmoja alitoroka kutoka Yerusalemu na kuja kwangu." Wababeli waliiangamiza Yerusalemu na kuwaua watu wa Yerusalemu, lakini watu walikimbia.

Mji ulikuwa umetekwa

"Wababeli wameuangamiza mji." Neno "mji" linairejea "Yerusalemu."

Mkono wa Yahwe ulikuwa juu yangu

Tazama tafsiri yake katika sura ya 1:1, "mkono wa Yahwe ulikuja juu yangu."

mapambazuko

"Mapambazuko" ni mda wa asubuhi sana wakati mwanga wa jua unapoanza kuchomoza.

kinywa changu kilifunuliwa

"Yahwe alifungua kinywa chake." "nitafungua kinywa chako"

sikuwa bubu tena

"niliweza kuzungumza sasa" Ezekieli hakuweza kuzungumza chochote isipokuwa maneno ya kinabii tangu 3:26.

Ezekiel 33:23

neno la Yahwe likaja

Yahwe akanena neno lake."

wale waishio mahali palipoharibika

"wale walio iharibu miji"

nchi

"nchi ya Israeli"

Tumepatiwa nchi

"Yahwe ametupatia nchi."

kama wamiliki

"ili tuweze kuimiliki" au "kama warithi."

Ezekiel 33:25

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na Ezekieli kuhusu watu waliokuwa wakiishi katika uharibifu wa Israeli.

Mmekula damu

Inaonekana kwamba wanakula damu kwa kula nyama ambayo bado inadamu ndani yake. "Manakula nyama yenye damu ndani yake."

mmeziinulia macho yenu sanamu

"mnazitegemea sanamu zenu." Hii inamaanisha kwamba "mnaziabudu sana zenu"

mnazimwagia damu za watu

"mnamwaga damu." Hii inamaanisha "mnawaua watu."

Je! mna uhakika wa kuimiliki hii nchi?

Yahwe anatumia hili swali kuwaonya watu. "Hamtakiwi kumiliki hii nchi" au "Hamstahili hii nchi."

Mnategemea upanga wenu

"Mmetumia upanga wenu kupata kile mnachokitegemea."

mmetenda mambo maovu

"tenda mambo ambayo ninayoyachukia sana"

kila mwanamume amemnajisi mke wa jirani yake

Inamaanisha kwamba wamewanajisi wake za majirani zao kwa kulala nao.

Ezekiel 33:27

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na ezekieli kuhusu watu waliokuwa wakiishi katika uharibifu wa Israeli.

Kama niishivyo

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:11.

anguka kwa upanga

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:11.

walio katika ngome na katika mapango watakufa kwa tauni

"tauni itawaua watu waishio katika ngome na mapango"

ngome

Ngome ni jengo ambalo watu hujenga kujilinda wenyewe na maadui wanao washambulia.

mapango

Mapango ni mashimo ya asili katika upande wa mlima au ndani ya aridhi.

na tishio

"Tishio" ni kitu ambacho kinwafanya watu kuogopa sana wanapokiona. "na watu wataogopa sana kwa sababu ya hiyo"

kiburi cha uweza wake kitaisha

Neno "yake" linarejea kwa nchi, ambayo inarejea kwa watu wa nchi. "watu wa nchi hawatajiinua tena kwamba wako hodari."

milima ya Israeli itakuwa jangwa

"hakuna atakayeishi katika milima ya Israeli"

hakutakuwa na mtu wa kupitia miongoni mwao

"hakutakuwa na yeyote atakaye achwa kusafiri kupitia kwenye nchi au juu ya milima"

mtajua yakwamba mimi ni Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 6:6.

wamemaliza

"watu wamemaliza"

machukizo yote waliyafanya

"mambo yote waliyafanya ninayachukia"

Ezekiel 33:30

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na Ezekili

Mwanadamu

Tazama tafsiri yake katika sura ya 2:1.

ile itokayo kutoka kwa Yahwe

"ile Yahwe aipelekayo"

Maneno ya hako hapo juu ya vinywa vyao

"maneno ya upendo yapo katika vinywa vyao"

mioyo yao inafuata udhalimu kwa faida yao

"katika mioyo yao wanataka kujipatia udhalimu" au "wanataka kujipatia vitu katika njia ambazo si sahihi."

Ezekiel 33:32

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na Ezekieli kuhusu watu wa Israeli.

wewe ni kama wimbo mzuri kwao

"wanafikiri kwamba wewe ni kama wimbo mzuri"

wimbo mzuri

Maana zinazowezekana "wimbo mzuri" au "wimbo wa mapenzi" au wimbo kuhusu mapenzi."

nzuri awezaye kucheza kinanda vizuri

"ambayo mtu hucheza vizuri kwenye kinanda kizuri."

wakati haya yote yatokeapo

Neno "haya" inarejea kwa mambo yote ambayo Mungu aliyasema yatatokea na kwamba Ezekieli aliwaambia watu.

tazama!

Neno "tazama" hapa linaongeza kusisitiza kwa kile kifuatacho.

yule nabii aliyekuwa miongoni mwao

"kwamba kweli nimekutumia nabii."

Ezekiel 34

Ezekiel 34:1

neno la Yahwe likaja

"Yahwe akanena neno lake."

wachungaji wa Israeli

Hili neno linawalinganisha viongozi wa Israeli ambao wanaotakiwa kuangalia watu wao pamoja na wachungaji ambao wanaotakiwa kuangalia kundi lao. "viongozi wa Israeli walio kama kondoo"

Tabiri na sema

Tazama tafsiri yake katika sura ya 21:8.

wanajichunga wenyewe

"wanajilisha na kujichunga wenyewe."

Je! wachungaji hawapaswi kulilinda kundi?

Yahwe anatumia hili swali kuwakaripia viongozi kwa kuacha kuwaangalia watu.

Mnakula mafungu yaliyonona

Inaonyesha kwamba fungu lililonona hutoka kwenye kondoo na mbuzi. "Mnakula sehemu za kondoo na mbuzi zilizonona"

"vaa sufu kutoka kondoo"

Mnachinja walionona

"Mnachinja mifugo wanene ili muweze kuwala"

wanene

"kondoo mwenye afya na mbuzi" au "kondoo na mbuzi walio nona kabia"

hamkuwalisha siku zote

"msiwalishe na kulichunga kundi"

Ezekiel 34:4

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa viongozi wa Israeli

wenye maradhi

"wanaumwa" au "wako dhaifu"

funga

"Hamuwafungi kuzungusha nguo vidonda na mifupa iliyovunjika"

wale waliovunjika

"kondoo waliovunjika mifupa" au "kondoo aliyeumia"

hamuwarudishi

"hamuwarudishi"

waliofukuzwa

"kondoo aliyekuwa amefunkuzwa" au "kondoo dhaifu amefukuzwa na kondoo shupavu"

aliyepotea

"kondoo au mbuzi aliyepotea"

kwa nguvu na vurugu

"kwa kulazimisha na kikatili"

bila mchungaju

"kwa sababu hawana mchungaji."

wakawa chakula kwa wanyama wote waishio katika mashamba

"wanyama wote wa porini waliwashambulia na kuwala"

limetawanyika juu ya uso wote wa dunia

"kundi langu limetwanyika juu ya dunia nzima"

Ezekiel 34:7

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa watu wa Israeli.

tangazo la Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:11.

Kama niishivyo

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:11.

hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:11.

kwa sababu kundi langu limekuwa mateka na chakula kwa ajili ya wanyama katika mashamba

"kwa sababu wanyama katika shamba wamekuwa wakiiba kundi langu na kuwala"

mateka

"vitu vilivyopotea.

wanyama katika mashamba

"wanyama wa porini"

kwa sababu hapakuwa na mchungaji

"kwa sababu hawana mchungaji"

wanajichunga wenyewe

"wanajichunga wenyewe"

hawakulilisha kundi langu

"hawakulilisha na kulichunga"

Ezekiel 34:9

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa viongozi wa Israeli.

Kwa hiyo, wachungaji, lisikilizeni neno la Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 34:7.

Tazama!

Neno "Tazama" hapa linaongeza msisitizo kwa kile kifutacho.

Niko juu ya wachungaji

"nitawaadhibu wachungaji."

nitalitaka kundi langu kutoka mkononi mwao

"nitawaadhibu kwa mambo yote mabaya waliyaacha kutokea kwa kundi langu."

nitawasitisha mbali na kuchunga kundi

"sitawaacha kulichunga kundi tena"

watajichunga wenyewe

"kujilisha na kujichunga wenyewe"

kutoka vinywani mwao

"hivyo hawataweza kuwala."

kundi langu halitakuwa chakula chao tena

"wachungaji hawatawala tena kondoo na mbuzi wa kundi langu"

Ezekiel 34:11

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendela kumptaia ezekieli ujumbe wake kwa viongozi wa Israeli.

Tazama!

Neno "Tazama" hapa linatahadharisha wachungaji kuwa makini kwa habari ifutayo ya kushangaza.

nitawatafuta

"nitawatafuta"

ndani ya kundi lake lililotawanyika.

"pamoja na kundi lake"

waliotawanyika

Kundi halipo sehemu moja. Kondoo na mbuzi wapo katika sehemu tofauti tofauti walipopotea na katika hatari.

katika siku ya mawingu na giza

"katika siku ya wingu na siku ya giza." Hii inarejea wakati majanga mengi yatakapo tokea. "wakati majanga mabaya yatakapowatokea."

warudishe

"rudisha kondoo na mbuzi wangu"

kutoka miongoni mwa watu

"kutoka mahali ambapo walipoishi pamoja na watu wengine"

malisho

nchi ambayo ina majani na mimea midogo ambayo kondoo na mbuzi wanaweza kula

makazi

sehemu ambapo watu huishi. Siku zote wanaishi katika nyumba za makazi.

Ezekiel 34:14

Maelezo ya Juma:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa viongozi wa Israeli

sehemu za malisho yao

"mahali ambapo wanaweza kula"

malisho mazuri

nchi zenye majana mengi na mimia

malisho

kula majani na mimea mingine

mimi mwenyewe

Neno "mimi mwenyewe" linaongeza msisitizo. Mungu atafanya hivi kwa sababu wachungaji hawakuwa wanafanya sahihi.

watalisha

"watalisha na kuwaangalia"

watawafanya kulala chini

"watawaacha walale chini"

hili ni tangazo la Bwana Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:11.

waliopotea

"wale waliopotea." "kondoo yeyote au mbuzi aliyepotea"

rudisha waliopotea

"kuwarudisha wale waliokuwa wamefukuzwa mbali"

funga kondoo aliyevunjika

"zungusha nguo kwa kondoo yeyote aliyevunjika mfupa"

Ezekiel 34:17

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake. Sasa ni watu wa Israeli.

tazama

Neno "tazama" hapa linaongeza msisitizo kwa kile kifuatacho.

nitakuwa hakimu kati ya kondoo

"nitakuwa hakimu kati ya kondoo, kondoo dume, na mbuzi"

kondoo dume na mbuzi dume

Kondoo dume na mbuzi huwa ni shupavu katika mifugo na wanaweza kufika popote watakapo kutoka wanyama wengine katika mifugo.

Haitoshi ... miguu

Huu ni mwanzo wa swali ambalo Mungu anatumia kukaripia wale shupavu kwa sababu si wakarimu kwa wale wadhaifu.

Ezekiel 34:20

Tazama!

Neno "tazama" hapa linaongeza msisitizo kwa kile kifuatacho.

mimi mwenyewe

Neno "nini mwenyewe" linasisitiza kwamba ni Yahwe ndiye atakaye hukumu.

nitahukumu kati ya kondoo mnene na yule mwembamba

"nitahakikisha kwamba kondoo mnene na mbuzi na kondoo wembamba na mbuzi wanatendeana kila mmoja vyema"

kwa ajili yako

"Neno "wewe" linarejea kwa kondoo na mbuzi ambazo hazikuwa zinawatenda vyema kondoo wengine na mbuzi.

kwa upande wako

"kwa upande wa mwili wako"

amewapiga

"amewasukuma"

kuwatawanya

"kuwafanya waende katika mahali tofauti tofauti"

mbali na nchi

"mbali na nchi ya Israeli"

Ezekiel 34:22

mateka

"vitu vilivypotea." Wachungaji na wanyama wa porini wamekuwa wakiiba kondoo na mbuzi kutoka kwa mifugo ya Yahwe.

nitahukumu kati ya kondoo mmoja na mwingine

Tazama tafsiri yake katika sura ya 34:17, "nitahukumu miongoni mwa kondoo."

Nitaweka juu yao mchungaji mmoja

"nitamtuma mchungaji mmoja kuwa kiongozi wa kondoo na mbuzi wangu"

mtumishi wangu Daudi

Yahwe amesema "Daudi" inarejea kwa uzao wa Dausi. "uzao wa mtumishi wangu Daudi."

nitakuwa Mungu wao

Tazama tafsiri yake katika sura ya 11:19.

atakuwa mwana mfalme miongoni mwenu

"atakuwa mtawala"

mimi, Yahwe, nimetangaza hivi

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:15.

Ezekiel 34:25

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa watu wa Israeli.

agano la amani

"agano lile liletalo amani"

wanyama waovu wa porini

Hawa ni wanyama wa porini ambao waliwaua kondoo na mbuzi.

Pia nitaleta baraka juu yao na juu ya maeneo yazungukao kilima changu

Baadhi ya matolea ya kisasa yanatafsiri "pia nitawarudisha na maeneo yanayozunguka kilima changu kwenye baraka."

katika wakati wake

"kwa wakati sahihi"

Hizi zitakuwa mvua za baraka

"Hii mvua itatolewa kama baraka"

na dunia itashindwa kuzaa matunda yake

"nchi itaotesha chakula" Chakula kitamea juu ya nchi

wataokoka

"watakuwa salama"

watajua yakwamba mimi ndimi Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 6:6.

fito za kongwa zao

"fito zinazoshikilia kongwa zao pamoja"

Ezekiel 34:28

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa watu wa Israeli.

mateka

Tazama jinsi ilivyo tafsiriwa katika sura ya 7:20.

sehemu ya kupanda nzuri

"bustani watakayo kuwa katika amani" au bustani ambayo itakuwa mashuhuri"

angamia kwa njaa

"njaa" au "au kuangamia kwa sababu ya ukosefu wa chakula:

Ezekiel 34:30

mimi, Yahwe Mungu wao, niko pamoja nao

"mimi, Yahwe Mungu wao, ninawasaidia"

Ni watu wangu

"na ni watu wangu"

hili ni tangazo la Yahwe

Tazama tafsiri yake ktika sura ya 5:11.

nitakuwa Mungu wako

"ndimi Mungu wako"

Ezekiel 35

Ezekiel 35:1

neno la Yahwe likaja

"Yahwe akanena neno lake."

Mwanadamu

Tazama tafsiri yake katika sura ya 2:1.

weka uso wako juu ya

Tazama tafsiri yake katika sura ya 4:1.

Mlima Seiri

"mlima Seiri." huu unarejea kwa wtu walioishi katika Edomu kwa sababu waliishi katika mlima Seiri. "watu wa Edomu"

kwa huo

"mlima" au "watu wa Edomu"

Tazama!

Neno "Tazama hapa linaongeza msisitiza kwa kile kifuatacho.

ni juu yako

Tazama tafsiri yake katika sura ya 21:1.

nitakupiga kwa mkono wangu

"nimeunyoosha mkono wangu juu yako." Hii inamaanisha "ni karibu kukushambulia."

ukiwa na tishio

Tazama jinsi ilivyo tafsriwa katika sura ya 33:27.

Ezekiel 35:4

Maelezo ya Jumla:

Huu ni mwendelezo wa ujumbe wa Yahwe kwa watu wa Mlima Seiri.

utajua yakwamba mimi ndimi Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 6:6.

umewatoa kwenye mikono ya upanga

"umewatoa juu ya maadui zao waliowaua kwa upanga" au "umewaua kwa upanga"

wakati adhabu yao

"katika kipindi wakati walipokuwa katika janga"

kama niishivyo

Tazama jinsi ilivyotafsiriwa katika sura ya 5:11.

hili ndilo tangazo la Bwana Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:11.

nitakuandaa kwa ajili ya damu

"nitakuandaa kwa kuipoteza damu yako." Hii inarejea kwa kujeruhuwa au kuuawa.

damu itakufuatilia

Yahwe anawakilisha damu kama mtu ambaye angewafukuza. "maadui zako wataendelea kukuchinja"

Kwa kuwa hukuichukia damu

"Tangu ulipoichukia wakati watu wengine walipouawa kikatili."

Ezekiel 35:7

Maelezo ya Jumla:

Huu ni mwendelezo wa ujumbe wa Yahwe kwa Mlima Seiri.

wakati nitakapoukatilia mbali kutoka huo yeyote apitaye na arudiye tena

"nitamwangamiza kila auingiaye au kuuacha"

waliouawa kwa upanga

Tazama jinsi ilivyo tafsiriwa katika sura ya 31:17.

mkiwa daima

"ukiwa daima" Hii ni kutia chumvi kusisitiza uharibifu.

Miji yako haitakaliwa

"watu hawataishi katika miji yako"

lakini mtajua

Hapa "ninyi" ni wingi. Mungu ananena na watu wa Mlima Seiri, kuliko na mlima mmoja.

mtajua kwamba mimi ni Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 6:6.

Ezekiel 35:10

Maelezo ya Jumla:

Huu ni mwendelezo wa ujumbe wa Yahwe kwa watu wa Milima Seiri.

Umesema

Neno "Wewe" linarejea kwa mlima wa Seiri ambao unawakilisha taifa la Edomu.

na sisi

Neno "sisi" linarejea watu wa Edomu.

hata wakati Yahwe alipokuwa pamoja nao

Inaonyesha kwamba Yahwe alikuwa akiilinda Israeli na Yuda. "Lakini Yahwe alikuwa huko akiilinda Israeli na Yuda"

kama niishivyo

Tazama jisni ilivyo tafsiriwa katika sura ya 5:1.

hili ndilo tangazo la Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:11.

itafanya kulingana na hasira yako na kulingana na wivu wako

"nitakuadhibu kwa sababu ya hasira yako na wivu"

Ezekiel 35:12

Maelezo ya Jumla:

Huu ni mwendelezo wa ujumbe wa Yahwe kwa watu wa Mlima .

watajua yakwamba mimi ndimi Yahwe

Tazama jinsi ilivyotafsiriwa katika sura ya 6:6.

wametolewa kwetu tuwale

"milima ya Israeli ni kwa aji yetu ili kutula" au tunaweza kuchukua chochote tutakacho kutoka kwao"

Ezekiel 35:14

Maelezo ya Jumla:

Huu ni mwendelezo wa ujumbe wa Yahwe kwa watu wa Mlima Seiri.

Bwana Yahwe asema hivi

Tazama tafsiri yake katika sura ya 3:10.

kufanya ukiwa

Neno "wewe" linarejea kwa "mlima Seiri ambao unawakilisha nchi ya Edomu. "nitaifanya nchi yako ukiwa."

nitakavyokutenda wewe

"nitaifanya nchi yako ukiwa" au "nitafanya shangwe wakati nchi yako ikiwa ukiwa"

Mlima Seiri

Tazama jinsi ilivyo tafsiriwa katika sura ya 35:1.

Kisha watajua

Neno "wao" yamkini linarejea kwa "watu wa dunia" au "watu wa Israeli na Yuda."

watajua kwamba mimi ndimi Yahwe

Tazama ilivyo tafsiriwa katika sura ya 6:6.

Ezekiel 36

Ezekiel 36:1

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na Ezekeili. Sasa ujumbe wake ni kwa milima ya Israeli.

mwanadamu

Tazama tafsiri yake katika sura ya 2:1.

tabiri juu ya milima ya Israeli

Mungu anamtaka Ezekilei kunena na milima kana kwamba walikuwa watu.

Enhe

Hii inaonyesha shangwa. Inaweza kutafsiriwa kama "nina furaha sana"

Mahala pa juu pa zamani

Hii inarejea kwa milima mirefu ya Israeli.

imekuwa milki yetu

"sasa ni mali yetu"

Kwa sababu ya ukiwa wenu

"Kwa sababu ninyi milima mmekuwa ukiwa"

kwa sababu mashambulizi yaliyokuja juu yenu kutoka pande zote

"kwa sababu mliishambulia kutoka kila mahali"

mmeambiwa kwa midomo yao waongeao, na kwa masingizio ya watu

"watu wanasema mambo mabaya kuhusu wewe, na mataifa wanasema hadithi mbaya kuhusu wewe"

midomo ya uzushi na ndimi

"maneno ya uzushi"

Ezekiel 36:4

Maelezo ya Jumla:

Huu ni mwendelezo wa ujumbe wa Yahwe kwa milima ya Israeli.

sikiliza neno la Bwana Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 6:1.

mahali palipoharibika kuwa ukiwa

"miji mikiwa ambayo hakuna watu wanaoishi katika hiyo"

miji iliyoachwa

"miji ambayo watu wamiacha nyuma"

imekuwa mateka

"hao maadui wamepotea"

huru kwa kutaniwa na mataifa yaliyowazunguka

"ambayo wengine, wanayoyazunguka mataifa wanadhihaki"

katika ghadhabu ya moto wangu

Yahwe anaipenda Israeili sana, hivyo amekuwa na wivu na hasira wakati mataifa mengine wanapoidhihaki.

juu ya Edom na wote

"na juu ya Edom yote"

wote walikuwa na shangwa katika moyo wao na dharau katika roho zao

"wameitukana watu wako Israeli.

shangwe katika moyo wake

"kwa shangwe katika mioyo yao"

dharau katika roho zao

inaonyesha kwamba dharau yao ni kwa ajili ya Israeli.

Tazama!

Neno "Tazama" hapa linaongeza msisitizo kwa kile kifuatach.

Katika ghadhabu yangu na hasira yangu

Maneno "ghadhabu" na "hasira" kimsingi yana maana moja. Yote yanasisitiza mkazo wa hasira.

mmechukua fedheha za mataifa

"mataifa mengine yamekufedhehesha"

Ezekiel 36:7

Maelezo ya Jumla:

Huu ni mwendelezo wa ujumbe wa Yahwe kwa mataifa ya Israeli.

Mimi mwenyewe nitainua mkono wangu kuapa

"mimi mwenyewe nitainua mkono wangu kuapa" Kuinua mkono inaonyesha kwamba kweli atafanya kile alicho kiapia'

kwamba mataifa yanayowazunguka yamkini yatawabebea aibu yao

"yamkini watu wakawadhihaki mataifa yaliyokuzunguka"

kuzunguka

Neno "wewe" linarejea kwa milima ya Israeli.

Ezekiel 36:8

Maelezo ya Jumla:

Huu ni mwendelezo wa ujumbe wa Yahwe kwa milima ya Israeli.

mtachipuza matawi na kuzaa matunda

"miti yenu itachipuza matawi na kuzaa matunda."

tazama

Neno "tazama" hapa linaongeza msisitizo kwa kile kinachofuata."

nipo kwa ajili yenu

"nataka kufanya mambo mazuri kwenu" Neno "ninyi" linarejea kwa milima ya Israeli.

na ninawatenda kwa fadhili

"nitakuwa mkarimu kwenu" (UDB)

mtalimwa na kupandwa mbegu

"Watu wangu, watalima aridhi yako na kuipanda mbegu." Kulima inamaanisha kukata matuta katika aridhi ili kupanda mbegu katika hiyo.

Ezekiel 36:10

Maelezo ya Jumla:

Huu ni mwendelezo wa ujumbe wa Yahwe kwa mataifa ya Israeli.

nyumba ya Israeli

Tazama tafsiri yake katika sura ya 3:1.

Miji itakaa na palipoharibiwa kujengwa

"Kisha watu wataishi katika miji na watayajenga tena magofu."

wataongezeka na kuzaa

"watakuwa watu wengi sana na watoto wengi sana"

nitawafanya kuishi kama mlivyokuwa

"watu kuishi juu yako milima kama walivyofanya kabla"

mtajua yakwamba mimi ni Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 6:6.

watakumiliki

Neno "wewe" ni umoja na linarejea kwa "nchi ya Israeli."

hutasababisha tena watoto wao kufa

Hii inaonyesha kwamba zamani watoto walikufa kwa sababu hapakuwa na chakula cha kutosha katika nchi. Kisha nchi ilizalisha chakula cha kutosha.

Ezekiel 36:13

Maelezo ya Jumla:

Huu ni mwendelezo wa ujumbe wa Yahwe kwa milima ya Israeli.

wanakwambia

"mataifa mengine yanakwambia milima"

Umewala watu

"Umewafanya watu wangu kufa." Neno "ume" ni umoja na linarejea kwa "nchi ya Israeli."

watoto wako wa taifa wamekufa

"umewafanya watoto wa watu wako kufa." Hii inaonyesha kwamba milima hufanya hivi kwa kuacha kuotesha mbegu nzuri.

Hili ndilo tangazo la Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:11.

Wala sintokuruhusu kusikiliza fedhiha za mataifa tena

"sitayaruhusu mataifa mengine tena kukufedhehesha."

hautachukua tena aibu ya watu

"watu hawatakusababisha kujisikia aibu"

au kufanya taifa lako kuanguka

"na ninyi milima fanyeni taifa lenu lishinde"

Ezekiel 36:16

neno la Yahwe likaja

"Yahwe akanena neno lake."

Mwanadamu

Tazama tafsir yake katika sura ya 2:1:

Nyumba ya Israeli

Tazama tafsiri yake katika sura ya 3:1.

pamoja na njia zao na matendo yao

"jinsi walivyoishi na mambo waliyoyafanya"

Njia zao zilikuwa kama uchafu wa hedhi ya mwanamke mbele yangu

"Njia zao zilikuwa kama machukizo kwangu kama uchafu wa hedhi ya mwanamke"

hedhi ya mwanamke

ni damu itokayo kwa mwanamke kila mwezi wakati anapokuwa hana mimba

nimeimwaga ghadhabu yangu juu yao

"nimefanya mambo kwao yanayoonyesha jinsi nilivyokuwa na hasira."

kwa ajili ya damu waliyoimwaga juu yanchi

"kwa sabababu wamefanya damu ya watu wengi kusambaa kwenye nchi" au "kwa sababu wamewaua watu wengi."

na kwa ajili ya uchafu wa hiyo kwa sanamu zao

"na kwa sababu wameinajisi nchi yangu kwa sanamu zao"

Ezekiel 36:19

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na Ezekieli kuhusu Israeli.

Nimewatawanya miongoni mwa mataifa; walitawanyika katika nchi tofauti tofauti.

Tazama tafsiri yake katika sura ya 12:14.

walitawanyika katika nchi tofautitofauti

"nimewatawanya kupitia nchi tofauti tofauti"

njia zao na matendo yao

"mambo ambayo waliyoyafanya"

wakati watu

"kwa sababu watu wengine wamesema"

nchi yake

Hii inarejea kwa nchi Israeli.

nalikuwa na huruma kwa ajili ya langu langu takatifu

"najali kusu jina langu." "nalitaka watu wajue kwamba mimi ndimi Yahwe."

nyumba ya Israeli

Tazama tafsiri yake katika sura ya 3:1.

Ezekiel 36:22

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na Ezekieli, na kumpatia ujumbe Israeli.

nyumba ya Israeli

Tazama tafsiri yake katika 3:1.

kwa ajili yako

"kwa sababu yako"

lakini kwa ajili ya jina langu takatifu

"ili watu wajue kwamba mimi ni mtakatifu"

mtajua kwamba mimi ndimi Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 6:6.

hili ni tangazo la Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:11.

Ezekiel 36:24

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa Israeli.

nyunyiza maji masafi

"kupitia maji masafi"

kutoka kwenye uchafu wako wote

"mambo yote yanayokufanya kuwa najisi"

Ezekiel 36:26

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa Israeli.

moyo mpya na roho mpya

Tazama tafsiri yake katika sura ya 11:19.

katika sehemu zenu za ndani

"ndani yenu"

moyo wa jiwe

Hii inalinganishwa na mioyo ya ukaidi na moyo wa jiwe.

nyama zako

"mwili wako"

mwili wa nyama

Huu ni moyo ambao sio mkaidi, lakini unatamani kumtii Mungu.

tembea katika maagizo yangu

Tazama tafsiri yake katika sura ya 11:9.

tunza maagiza yangu, hivyo utawafanya

"utayashika maagizo yangu na kuyafanya"

watu wangu

Tazama tafsiri yake katika sura ya 11:19

Ezekiel 36:29

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa Israeli.

nitatia unga

"nitaita unga uje" Hili neno linawakilisha unga kama mtumishi wa Yahwe.

hamtazaa tena aibu ya njaa miongoni mwa mataifa

"mataifa hayatakufanya kujisikia aibu kwa sababu mnateseka na njaa"

matendo maovu

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:9.

Ezekiel 36:32

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa Israeli.

kwa ajili yako

"kwa ajili yako"

hili ndilo tangazo la Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:11.

ijulikane kwenu

"unaweza kuwa na uhakika na hili"

Hivyo tahayarikeni na kufadhaika

Maneno "tahayarika" na "kufadhaika" yana maana moja. Yote yanasisitiza mkazo wa tahayari.

kwa sababu ya njia zako

"kwa sababu ya kile ufanyacho"

nyumba ya Israeli

Tazama tafsiri yake katika sura ya 3:1.

mtailima nchi iliyoharibiwa

"mtailima nchi iliyoharibiwa"

mbele za macho ya wote wapitao karib

"na wasafiri wote katika nchi wataiona"

Ezekiel 36:35

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa Israeli.

Kisha waka

Neno "waka" llinarejea kwa watu wanaotembea kupitia nchi ya Israeli.

palipokuwa pamebomolewa

"maadui walipaangusha chini"

watajua yakwamba mimi ndimi Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 6:6.

kwamba nimeyajenga magofu

"na kuijenga miji ambayo maadui walipokuwa wamepabomoa"

kuipanda mbegu sehemu zilizokuwa ukiwa

"kupanda mbegu katika nchi kiwa"

Ezekiel 36:37

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na Ezekieli.

kuwaongeza kama kundi la watu

"kuwafanya kama kundi la kondoo." Kondoo huongezeka haraka. kuwafanya watu kuongezeka haraka kama kondoo."

watajua kwamba mimi ndimi Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 6:6.

Ezekiel 37

Ezekiel 37:1

Maelezo ya Jumla:

Ezekieli ananena

Mkono wa Yahwe ulikuwa juu yangu

Tazama tafsiri yake katika sura ya 1:1, "mkono wa Yahwe ukaja juu yangu."

katikati

"katikati"

kuzunguka pote

"katika kila mahali"

Tazama!

Neno "Tazama" hapa linatutahadharisha kuwa makini kwa habari zifuatazo za kushangaza.

mwandamu

Tazama tafsiri yake katika sura ya 2:1.

Ezekiel 37:4

Maelezo ya Jumla:

Yahwe ananena na Ezekieli.

Sikiliza neno la Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 13:1.

Tazama

"Ona" au "Sikia"

mishipa

sehemu ya miili ya mwanadamu ambayo ni kama gidamu ngumu na hushikkamana na mifupa na misuli pamoja

weka pumzi miongoni

Hapa "pumzi" inarejea kwa kupumua. "nitakufanya kupumua"

pumzi

Neno la Kiebrania limetafsiriwa kama "pumzi" katika mstari huu limetafsiriwa kama "roho" pia limetafsiriwa katika matoleo mengine machache kama "upepo"

mtajua kwamba mimi ndimi Yahwe

Tazama tafsiri yakekatika sura ya 6:6.

Ezekiel 37:7

Maelezo ya Jumla:

Ezekieli ananena

kama nilivyokuwa nimeamuru

"kama yahwe alivyokuwa ameniamuru kunena."

tazama

Neno "tazma" hapa linaonyesha kwamba ezekieli alishangazwa kwa kile alichokiona.

mishipa

Hii inarejea kwa sehemu za binadamu ambazo ni kama gidamu ngumu na kushika mifupa na misuli pamoja.

Lakini hapakuwa na pumzi juu yao

Hapa "pumzi" inarejea kwa tendo la kupumua. "lakini hawakuwa wanapumua" au "hawakuwa hai"

Ezekiel 37:9

mwanadamu

tazama tafsiri yake katika sura ya 2:1.

pumzi

"pumzi" au "roho" au "upepo"

kutokakwenye pepo nne

"kutoka pande ambazo upepo unaweza kuvuma" au "kutoka kila upande"

hawa waliouwa

"hawa watu ambao ni maadui na maafa wameawa."

kama nilivyokuwa nimeamuru

"kama Yahwe alivyo niamuru"

Ezekiel 37:11

mwanadamu

Tazama tafsiri yake katika sura ya 2:1.

nyumba yote ya Israeli

Tazama tafsiri yake katika sura ya 3:1.

Tazama!

Neno "Tazama" hapa linaongeza kusisitiza kwa kile kifuatacho.

tabiri na sema

Tazama tafsiri yake katika kumbu ya bibilia 21:08.

Tazama

"Ona" au "Sikia"

Ezekiel 37:13

Maelezo ya Jumla:

Haya ni maneno ya Yhawe kwa watu wa Israeli.

watajua yakwamba mimi ndimi Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 6:6.

mabaki ya nchi yako

"kuishi kwa amani katika nchi yako mwenyewe"

hili ni tangazo la Yahwe

Tazama jinsi ilivyo tafsiriwa katika sura ya 5:11.

Ezekiel 37:15

neno la Yahwe likaja

"yahwe akanena neno lake." Tazama tafsiri yake katika sura ya 1:1.

mwanadamu

tazama tafsiri yake katika sura ya 2:1.

Kwa ajili ya Yuda

"Inawakilisha Yuda"

Yuda

Kabila la Yda liliishi uapande wa utawala wa kuskazini mwa Israeli ambayo iliitwa Yuda. hapa hili jina limetumika kurejea ufalme wote wa kusini.

watu wa wote Israeli, wenzake

Hii inarejea kwa Waisraeli walioishi katika ufalme wa kusini mwa Yuda.

Efraimu

Kabila la Efraimu liliishi katika ufalme wa kusini mwa Israeli. Hapa hili jina limetumika kurejea ufalme wote wa kaskazini.

watu wote wa Israeli, wenzao

Hii inarejea kwa Waisraeli walioishi upande wa ufalme kaskazini mwa Israeli.

kwenye fimbo moja

"ili kwamba wawe fimbo moja"

Ezekiel 37:18

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na Ezekili.

watakaponena na wea na kusema

Tazama tafsiri yake katika sura ya 33:23.

haya mambo yako yana maana gani

"fimbo zako nina maana gani" au "kwa nini upo na hizi fimbo"

Tazama!

"Ona" au "Sikia!"

chipukizi la Yuda

"chipukizi la Yuda." Hii inawakilisha utawala wa Israeli.

lipo kwenye mkono wa Efraimu

Neno "mkono" linarejea kwa uweza. "ambalo ni kabila la Efraimu kutawala"

kabila za Israeli wenzake

"makabila mengine ambayo ni wenzao na Israeli. au "makabila mengine ya Israeli ambayo ni sehemu ya huo ufalme"

tawi la Yuda

"fimbo ya Yuda." Hii inawakilisha ufalme wa yuda.

mbele ya macho yao

Tazama tafsiri yake katika sura ya 21:16.

Ezekiel 37:21

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na Ezekilei.

Tazama!

"Ona!" au "Sikia!"

mambo ya machukizo

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:11.

watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao

tazama tafsir yake katika sura ya 11:19.

Ezekiel 37:24

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kunena na Ezekieli.

Daudi mtumishi wangu

Tazama tafsiri yake katika sura ya 34:22.

juu yao

"juu ya watu wa Israeli"

mchungaji mmoja juuyao

tazama tafsiri yake katika sura ya 34:22.

wataenenda kulingana na amri zangu

"wataishi kama nilivyo amuru"

watazitunza amri zangu na kuzitii

Tazama tafsiri yake katika sura ya 18:19.

alikaa

"aliishi"

mkuu

"mwana mfalme"

Ezekiel 37:26

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anazungumzia kuhusu watu wa israeli.

Nitaanzisha agano

"nitaweka"

agano la amani

Tazama tafsiri yake katika sura ya 34:25.

nitayaimarisha

Inaonyesha kwamba Yahwe wangeweza kuwaimarisha katika nchi ya Israeli.

zidisha

Tazama tafsiri yake katika sura ya 36:10

mahali pangu patakatifu

"patakatifu pangu" au "hekalu langu"

makao yangu

"mahali ambapo ninaposhi"

nitakuwa Mungu wao, na wao watakuwa watu wangu

Tazama tafsiri yake katika sura ya 11:19.

watajua yakuwa mimi ndimi Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 6:6.

mahali pangu patakatifu

"patakatifu pangu" au "hekalu langu"

kati yao

"miongoni mwao"

Ezekiel 38

Ezekiel 38:1

Neno la Yahwe likaja

"Yahwe akanena neno lake."

Gogu

Hili ni jina la kiongozi au mfalme aliyetawala katika nchi ya Magogu.

nchi ya Magogu

Inaonyesha kwamba hii ni nchi ambayo Gogu alitawala.

Magogu

jina la zamani la taifa ambalo kwa sasa ni Uturuki.

kiongozi mkuu wa Mesheki na Tubali

Usemi huu umetokea mara mbili katika mistari hii.

Ezekiel 38:4

Maelezo ya jumla:

Yahwe ananena na Gogu

weka ndoana katika taya yako

Watu huweka ndoana katika midomo ya wanyama ili waweze kuongoza wanyama popote watakapo.

Puti

taifa lililoishi katika mahali ambapo ni Libya kwa sasa.

Beth-Togarma

Tazama tafsiri yake katika sura ya 27:14.

Ezekiel 38:7

Maelezo ya Jumla:

Yahwe ananena na Gogu.

Utaitwa

"nitakuita kuta kwa ajili ya vita."

makundi yako ya jeshi yatakusanyika pamoja nawe

"makundi yako yote ya jeshi ambayo umeyakusanya kwako"

uliyokuwa umeyakusanya

"na wale watu uliowakusanya."

Ezekiel 38:10

Itakuwa siku hiyo hayo

"katika kipindi hicho"

mawazo yataingia katika mioyoni yenu

"mawazo yatakuja kwenye akili zenu"

Ezekiel 38:13

Maelezo ya Jumla:

Yahwe ananena na Gogu.

Sheba

Tazama tafsiri yake katika sura ya 27:22.

Denani

Tazama tafsiri yake katika sura ya 25:12.

mifugo

kondoo, mbuzi, ng'ombe

Ezekiel 38:14

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa Gogu.

Katika siku hiyo ... jifunze kuhusu wao

Yahwe anatumia hili swali kusisitiza kwamba Gogu atasikia hasa kuhusu watu wanaoishi katika Israeli.

wanaweza kunijua

"wanaweza kunijua mimi ni nani"

Ezekiel 38:17

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe kuhusu Gogu.

e, wewe siye yule ambaye ... yao?

Yahwe anatumia hili swali kusisitiza kwamba ni yeye ndiye aliyekuwa amemleta Gogu kwenye nchi ya Israeli.

yule ambaye niliyeongea naye

"ambaye ninaye mzungumzia"

juu yao

"juu ya watu wa Israeli"

Ezekiel 38:19

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe kuhusu Gogu.

Milima itaangushwa chini

"Yahwe ataifanya milima kuanguka chini."

Ezekiel 38:21

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa gogu.

natafurika mvua, na mvua ya mawe ya moto. Nitaleta mvua ya kiberiti

"na nitanyeshea nchi mafuriko ya mvua, mvua ya mawe na kuchoma salfa"

mvua ya mawe

barafu ambayo huanguka chini kutoka angani

kiberiti

"salfa"

nitaonyesha ukuu wangu na utakatifu wangu

"onyesha kwamba mimi ni mkubwa na mtakatifu"

Ezekiel 39

Ezekiel 39:1

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe kwa Gogu.

Tazama!

"Ona" au "Sikia!"

mkuu wa Mesheki na Tubali

Haya maelezo yalitokea mara mbili katika hii mistari.

Ezekiel 39:4

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatiak Ezekieli ujumbe kwa Gogu.

Magogu

Tazama tafsiri yake katika sura ya 38:1.

watajua ya kwamba mimi ni Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 6:6.

Ezekiel 39:7

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpattia Ezekieli ujumbe wake kwa Gogu.

nitalifanya jina langu takatifu lijulikane kati ya watu wangu Israeli

"nitawafanya watu wangu, Israeli, kujua jina langu takatifu."

Tazama!

"Tazama!" au "Sikia!"

Ezekiel 39:9

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia ezekieli ujumbe wake kuhusu Gogu.

rungu

mbao zilizotengenezwa kwa mbao kama silaha

watawateka nyara

tazama tafsiri yake katika sura ya 23:46.

Ezekiel 39:11

Maelezo ya Jumala:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kuhusu Gogu.

itakuwa ... kwamba

tukio la mihimu litafanywa.

magharibi mwa bahari

matoleo ya kisasa yanatafsiri maelezo ya Kiebrania hapa kama "upande wa magharibi kuelekea bahari."

Itazuia

"jefu lililokufa litazuia"

Huko wata

"Huko nyumba ya Israeli"

Watapaita

"Watu watapaita"

bonde la Hamon-Gogu

"Bonde la Jeshi Kubwa la Gogu"

Ezekiel 39:12

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kuhusu Gogu.

mwezi wa saba

"mweza wa 7"

kuwazika

"kuwazika watu wa jeshi la gogu"

hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:11.

Ezekiel 39:14

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kuhusu Gogu.

kupitia nchi

"kupitia nchi ya Israeli"

Hamoni

Hili ni jina la "Jeshi Kubwa."

Ezekiel 39:17

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia ujumbe wake kwa ndege na wanyama wa porini.

kwenye sadaka

"kwenye karamu" au "kuchinja" Yahwe alimaanisha kwamba atawapatia ndege na wanyama chakula kizuri na sio kuwaabudu.

wote walikuwa wanene katika Basheni

"wote wakawa wanene wakati wakiwa wanachunga Basheni."

Ezekiel 39:19

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa ndege na wanyama wa porini.

farasi

"watu ambao huendesha farasi."

hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:11.

Ezekiel 39:21

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kuhusu Gogu.

Nitauweka utukufu wangu kati ya mataifa

"nitayafanya mataifa kuona utukufu wangu"

hukumu yangu ninayoionyesha na mkono wangu nimeuweka juu yao

Maneno haya yote yanarejea kwa hukumu ambayo Yahwe ataadhibu juu ya Israeli.

mkono wangu

Hapa neno "mkono" inarejea uweza wa Yahwe ambao huutumia kuleta hukumu.

juu yao

"juu ya watu wa jeshi kubwa la Gogu"

Ezekiel 39:23

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe kuhusu Gogu.

naficha uso wangu

"niliacha kuwalinda na kuwajali."

anguka kwa upanga

Tazama tafsiri yake katika sura ya 32:22.

Ezekiel 39:25

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kuhusu nyumba ya Israeli.

nitawarudisha watu wa Yakobo

Tazama tafsiri yake katika sura ya 16:53.

uhaini

"-sio aminifu"

nitajifunua mimi mwenyewe kuwa mtakatifu kwenye uso wa mataifa mengi

"mataifa mengi watajua kwamba mimi ni mtakatifu kwa sababu ya kile kilichofanyika kwa nyumba ya Israeli."

Ezekiel 39:28

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kuhusu nyumba ya Israeli.

wakati nitakapomwaga Roho wangu juu ya nyumba ya Israeli

"wakati nitakapoijaza nyumba ya Israeli ujazo wa Roho wangu"

Ezekiel 40

Ezekiel 40:1

miaka ishirini na tano ... miaka kumi na nne

miaka mitano ... miaka kumi na nne -

ya utumwa wetu

Hapa "yetu" inamrejea Ezekieli na Waisraeli ambao walikuwa katika Babeli tangu kipindi Wababeli walipomlazimisha Mfalme Yehoyakini kuondoka Yerusalemu.

mwanzoni mwa mwaka siku ya kumi ya mwezi

Huu ni mwezi wa kwanza wa kalenda ya Kiebrania. Siku ya kumi ipo katika Mwezi wa nne kwa kalenda za Magharibi.

mji ulitekwa

"Wababeli waliuteka mji wa yerusalemu"

mkono wa Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 1:1.

Akanileta kupumzika

"Akaniweka chini"

Ezekiel 40:3

akanipeleka huko

Yahwe akanileta hata mahali ambapo palipokuwa na majengo"

Tazama

Neno "tazama" hapa linaonyesha kwamba Ezekieli alishangazwa kwa kile alichokiona.

mshipi wa kitani

"ni kama iliyotengenezwa kwa kitani." Hiki ni kifaa kwa ajili ya kupimia umbali mrefu.

fimbo ya kupimia

Hiki ni kifaa kwa ajili ya kupimia umbali mfupi.

Mwanadamu

Tazama tafsiri yake katika sura ya 2:1.

elekeza moyo wako juu

"fikiri kuhusu."

nyumba ya Israeli

Tazama tafsiri yake katika 3:1

Ezekiel 40:5

kuzunguka eneo la hekalu

"kuelekea moja kwa moja kuzunguka eneo la hekalu"

dhiraa sita urefu

"dhiraa sita urefu." Hii ilikuwa kama mita 3.2.

kila "urefu" unalingana na dhiraa na ujazo wa kiganja

Kila urefu wa dhiraa ulikuwa kama sentimita 54.

ujazo wa kiganja

"upana wa mkono." Hii ilikuwa kama sentimita 8.

upana wa ukuta

"ni jinsi gani ukuta ulikuwa mpana." Ukuta ulikuwa mpana kama jengo.

mwanzi mmoja

"ilikuwa mwanzi mmoja upana." Hii ni kama mita 3.2.

urefu mwanzi mmoja

"na mwanzi mmoja urefu"

panda ngazi zake

"na alipanda ngazi za lango"

kina

"kutoka mbele ya kizingiti hata nyuma"

vyumba vya ulinzi

Kulikuwa na vyumba vilivyokuwa vimejengwa ndani ya lango ambavyo walikaa walinzi kulinda lango.

dhiraa tano

kama mita 2.7.

kati ya vyumba viwili

"kati ya vyumba"

varanda

Tazama tafsiri yake katika sura ya 8:16.

Ezekiel 40:8

varanda

Tazama tafsiri yake katika sura ya 8:16.

mwanzi mmoja

Tazama tafsiri yake katika sura ya 40:5.

dhiraa mbili

Kama mita moja.

dhiraa

Tazama tafsiri yake katika sura ya 40:5.

kipimo kile kile

"vilikuwa kipimo kimoja"

Ezekiel 40:11

lango la kuingia

"uwazi uliokuwa lango la kuingilia"

dhiraa kumi

kama mita 5.4.

dhiraa kumi na tatu

kama mita 7

vyumba vya ndani

"vyumba"

dhiraa sita

kama mita 3.2

dhiraa moja

"mita 54"

dhiraa ishirini na tano

dhiraa tano - kama mita 13.5

ambacho ni cha pili

"lango la pembe ya pili"

Ezekiel 40:14

vyumba ya ulinzi

Tazama tafsiri yake katika sura ya 40:5.

dhiraa sitini

kama mita thelathini na mbili.

dhiraa

Tazama tafsiri yake katika sura ya 40:5.

varanda

Tazama tafsiri yake katika sura ya 8:16.

dhiraa hamsini

kama mita ishini na saba

madidirsha yote yalikuwa upande wa ndani

"madirisha yalikuwa yamezunguka upande wa ndani"

Ezekiel 40:17

uwanja wa ndani

Tazama tafsiri yake katika sura ya 10:3.

Tazama!

Neno "Tazama" hapa linatuonyesha kwamba Ezekieli ameona kitu kinachovutia.

kibamba

sakafu iliyo sawa swa iliyotengenezwa kwa matofali

pamoja navyumba thelathini karibu na kibamba

"na kulikuwa na vyumba thelathini vyote vimezunguka kibamba."

kupanda kuelekea

"kwenda moja kwa moja kuelekea"

dhiraa mia moja

Kama mita hamsini na nne.

dhiraa

Tazama tafsiri yake katika sura ya 40:5.

Ezekiel 40:20

chumba cha ndani

Tazama tafsiri yake katika 40:5.

kivaranda

Tazama tafsiri yake katika 8:16.

kipimo kile kile

"kulikuwa na kipimo kile kile"

dhraa hamsini

kama mita ishirini na saba.

dhiraa

Tazama tafsiri yake katika sura ya 40:5.

dhiraa ishirini na tano

dhiraa tano -kama mita 13.5

lango kuu

lango ambalo lilikuwa upande wa magharibi mwa hekalu

Ezekiel 40:22

Maelezo ya Jumla:

Ezekieli anaendelea kuelezea maono ya hekalu na ya yule mtu anayefanana na shaba.

Madirisha yake

Neno "yake" inarejea kwa lango ambalo lilikuwa upande wa kusini mwa uwanja wa nje.

vyumba vya ndani

Tazama tafsiri yake tatika sura ya 40:5.

ilikabiliana na lango lililoelekea mashariki

"ilikuwa kama lile lango lililoelekea mashariki"

uwanja wa ndani

Tazama tafsiri yake katika sura ya 8:16.

mbele ya lango linaloelekea kaskazini

"moja kwa moja kukatiza kutoka lango linaelekea kaskazini"

pia kama kulikuwa na lango kuelekea magharibi

"pia kama kulikuwa na lango lililokuwa limeelekea uwanja wa ndani mbele ya lango kuelekea magharibi"

lango moja kuelekea jingine

"kutoka lango la nje upande wa kaskazini kuelekea lango la ndani upande wa kaskazini"

dhiraa

Tazama tafsiri yake katika sura ya 40:5.

dhiraa mia moja

kama mita hamsini na nne

Ezekiel 40:24

kama lango jingine la nje

"kama hayo ya kaskazini na malango ya magharibi"

dhiraa

Tazama tafsiri yake katika 40:5.

dhiraa hamsini

Kama mita thelathini na saba.

dhiraa ishirini na tano

dhiraa tano -kama mita 13.5.

Ezekiel 40:26

varanda

tazama tafsiri yake katika 8:16

dhiraa

Tazama tafsiri yake katika 40:5.

dhiraa mia moja

kama mita hamsini na tano.

Ezekiel 40:28

ua wa ndani

Tazama tafsiri yake katika 8:16.

vyumba vya ndani

Tazama tafsiri yake katika 40:5.

varanda

Tazama tafsiri yake katika 8:18.

dhiraa

Tazama tafsiri yake katika 40:5.

dhiraa hamsini

kama mita 27.

dhiraa ishirini na tano

dhiraa tano -kama mita 13.5

dhiraa tano

kama mita 2.7

Hii varanda ilielekea ua wa nje

"varanda ilikuwa mbele ya ua wa nje." Watu wangeweza kwenda ndani na nje yake kutoka kwenye ua.

pamoja na mitende

"na ilikuwa na mapango ya mitende"

Ezekiel 40:32

dhiraa

Tazama tafsiri yake katika 40:5.

dhiraa hamsini

kama mita ishirini na saba.

dhiraa ishirini na tano

dhiraa tano - kama mita 13.5

Ezekiel 40:35

dhiraa

Tazama tafsiri yake katika 40:5.

dhiraa hamsini

kama mita ishirini na saba.

dhiraa ishirini na tano

dhiraa tano - kama mita 13

Ezekiel 40:38

karibu na kila lango la ndani

"katika kila malango ya ndani"

walipooshea sadaka za kutekezwa

Neno "wao" linarejea kwa watu au makuhani waliokuwa wakileta sadaka.

pande zote

"pande zote"

sadaka ya kuteketezwa ilipochinjiwa

"walijinja sadaka ya kuteketeza" au "waliua wanya ambao wangeteketezwa kama sadaka."

Ezekiel 40:42

jiwe lililochongwa

"ambalo lilikuwa limetengenezwa kwa jiwe ambalo lililokuwa limekatwa"

dharaa

Tazama tafsiri yake katika 40:5.

dhiraa moja na nusu

Kama mita 0.8.

dhiraa moja

kama nusu mita

Kulabu mbili ujazo wa kiganja urefu uliokuwa umeunganishwa katika ua pande zote

"Kuzunguka varanda yote, watu walikuwa wameshambulia ndoana zilizokuwa zimejaa mkono mrefu na vidole viwili kila kimoja"

Kulabu mbili

kitu ambacho hatua mbili za tao, ambayo watu watu wanaweza kuning'niza vitu juu

ujazo wa kiganja urefu

kama mita nane.

nyama ya matoleo ilikuwa imewekwa juu ya meza

"wataweka mwili wa sadaka juu ya meza

Ezekiel 40:44

lango la ndani

Hili ni lango la ndani upande wa kaskazini.

vyumba vya waimbaji

"vyumba vya waimbaji"

Hiki chumba kilichoelekea kusini

Hili neno linamaanisha "Chumba chenye lango lake la kuingia kwa upande wa kusini."

nani yu katika zamu katika hekalu

"nani anafanya kazi katika hekalu" au "nani anawajibika kwa ajili ya kulinda hekalu"

Ezekiel 40:46

Maelezo ya Jumla:

Yule mtu anaendelea kunena na Ezekieli katika maono

chumba kinachoelekea kaskazini

"ambacho kilikuwa na lango la kuingia upande wa kaskazini"

yeye

"yule mtu"

dhiraa

Tazama tafsiri yake katika 40:5.

dhiraa mia moja

Kama mita arobaini na nne.

pamoja na madhabahu

"na ilipokuwa madhabahu"

nyumba

Hii inarejea kwa hekalu.

Ezekiel 40:48

varanda

Tazama tafsiri yake katika 8:6.

mhimili wake

"mhimili wa nyumba"

dhraa

Tazama tafsiri yake katika 40:5, "refu."

dhiraa mbili

kama mita 2.7

dhiraa kumi na nne

kama mita 7.5

dhiraa tatu

kama mita 1:6

dhiraa ishirini

kama mita kumi na saba

dhiraa kumi na moja

kama mita sita

nguzo

vipande vya mawe ambavyo ni virefu na vyembamba na kusaidia majengo

Ezekiel 41

Ezekiel 41:1

Maelezo ya Jumla:

Yule mtu katika maono ya Ezekieli (40:) anaendelea kumuonyesha Ezekieli kuzunguka hekalu.

Ezekiel 41:3

dhiraa

Tazama tafsiri yake katika sura ya 401:5 "urefu"

hata mbele ya ukumbi wa hekalu

"kama upana wa mahali patakatifu"

Ezekiel 41:8

fimbo nzima

Tazama tafsiri yake katika sura ya 4:5, "fimbo"

Ezekiel 41:10

vyumba vya pembeni vya kuhani

"vyumba vya pembeni vya makuhani vilikuwa mbali na patakatifu"

Ezekiel 41:12

lazimisha

Tazama tafsiri yake katika sura ya 40:28.

Ezekiel 41:15

juu

"ubaraza wa ghorofa." Ubaraza wa ghorofa palikuwa mahali palipokuwa pamejengwa juu kuliko sehemu nyingine za jengo. Watu wanaweza kwenda kwenya ubaraza wa ghorofa na kutazama chini upande wa sakafu ya jengo.

varanda

Tazama tafsiri yake katika sura ya 8:16.

Ezekiel 41:18

pamba

kufanya kitu kuwa kizuri hasa kwa kuweka kitu juu yake

nyumba

"patakatifu"

Ezekiel 41:21

Kulikuwa na milango miwili kwa ajili ya mahali patakatifu na mahali patakatifu sana

"mahali patakatifu na patakatifu sana kote kulikuwa na milango miwili"

Hii milango ilikuwa na bawaba mbili zilizokuwa zimeshikilia paneli za mlango yote

"Kila mlango ulikuwa na sehemu mbili katika bawaba." Bawaba inaunganisha milango kwenye ukuta na kuruhusu milango kubembea.

paneli mbili kwa ajili ya mlango mmoja na paneli mbili kwa ajili ya mwingine

"milango yote kwa sehemu zote mahali patakatifu na mahali pa juu sana palikuwa na sehemu mbili"

Ezekiel 41:25

kama kutu zilivyokuwa zimepambwa

"kama vile pia kuta zilivyokuwa na mapango ya kerubi na minazi"

varanda

Tazama tafsiri yake katika sura ya 8:16.

Ezekiel 42

Ezekiel 42:1

ua wa nje

Tazama tafsiri yake katika sura ya 10:3.

ua wa ndani

Tazama tafsiri yake katika sura ya 8:16.

na palikuwa pamefunguliwa kwa ajili yao

"na palionekana nje kwenye ua wa ndani"

kuwa na njia ya kutembea

"kwa sababu kulikuwa na mahali ambapo ungeweza kutembea karibu na vyumba"

Ezekiel 42:4

kiasi kidogo kulinganisha na vyumba

"ndogo kuliko vyumba"

Ezekiel 42:7

kuelekea

Tazama tafsiri yake katika sura ya 40:8.

Ezekiel 42:10

kwenye kichwa chake

"mwanzo wake"

Ezekiel 42:13

sadaka ya chakula

Hii ilikuwa sadaka ya unga. Watu walitoa "sadaka ya chakula" kuonyesha walikuwa na shukrani kwa Mungu.

Ezekiel 42:16

Alipima

Neno "ali" linarejea kwa yule mtu aliyefanana na shaba.

Ezekiel 42:20

Ilikuwa na ukuta umeizunguka ilikuwa dhiraa

"Nyumba ilikuwa na ukuta umeizunguka ambao ulikuwa na urefu."

Ezekiel 43

Ezekiel 43:1

Tazama!

Neno "tazama" hapa linatutahadharisha kuwa makini kwa habari ya kushangaza inayofuata.

kama mlio wa maji mengi

Tazama tafsiri yake katika sura ya 1:24, "Kama sauti ya maji yanayotiririka.

nchi iling'aa

"nchi ilikuwa na mg'ao wa mwanga"

Ezekiel 43:3

Lilikuwa kama

Neno "lili" inarejea kwa maono ya utukufu wa Mungu unaokuja kutoka mashariki.

wakati alipokuja kuiangamiza nchi

"wakati Mungu wa Israeli alipokuja kuuangamiza mji"

Ezekiel 43:6

mizoga ya wafalme wao

Hapa "mizoga" inarejea kwa sanamu ambazo watu wa wafalme waliziabudu. Sanamu zinaitwa mizoga kwa sababu zimekufa haziko hai.

Wameasi

"Nyumba ya Israeli imeasi"

matendo ya machukizo

Tazama jinsi ilivyo tafsiriwa katika sura ya 5:9.

nimewala kwa hasira yangu

Hili neno linamaanisha "nimewaangamiza kabisa kwa sababu nilikuwa na hasira."

Ezekiel 43:9

mizoga ya waflme wao

Hapa "mizoga" inarejea kwa sanamu ambazo watu wa wafalme waliziabudu. Sanamu zinaitwa mizoga kwa sababu haziko hai.

Ezekiel 43:10

namna

"hii mbinu"

mbele ya macho yao

Tazama tafsiri yake katika sura ya 21:6

watatunza ubunifu wake wote

"watatunza kiolezo"

Ezekiel 43:12

maelekezo

"kanuni"

mipaka inayozunguka

Neno "mpaka" ni kama linarejea kwa ukuta ulioelekea moja kwa moja kuzunguka hekalu.

takatifu sana

"takatifu hasa"

Tazama!

Neno "Tazama" hapa linasisitiza kwa kile kifuatacho.

Ezekiel 43:13

Mpaka unaozunguka machinjio

"Mpaka unaoelekea kuzunguka machinjio yake"

Hii ilikuwa chini ya madhabahu

"Hivi vilikuwa vipimo vya chini ya madhabahu."

chini ya madhabahu

"chini kusaidia madhabahu" au "msingi wa msingi wa madhabahu"

Ezekiel 43:15

Moyo

mahali ambapo dhabihu ambapo pengine zilipikwa au kuchomwa kwa moto

pembe

Pembe zilikuwa ni sehemu za madhabahu kwenye pembe ya madhabahu zinazoshikilia juu sehemu nyingine za madhabahu.

Ezekiel 43:18

alisema

"Yahwe alisema"

Mwanadamu

Tazama tafsiri yake katika sura ya 2:1.

taratibu

"sheria" au "maelekezo"

Uta

Neno "uta" ni umoja.

Ezekiel 43:20

Kisha utachukua

Tazama tafsiri yake katika sura ya 43:18.

pembe nne

Tazama jinsi ilivyo tafsiriwa katika sura ya 43:15.

Ezekiel 43:22

katika siku ya pili ume

Tazama tafsiri yake katika sura ya 43:18.

Vitoe mbele ya Yahwe

Madhabahu ambayo watatoa ng'ombe dume na kondoo dume, i mbele ya Hekalu ambapo uwepo wa Yahwe ulipo.

Ezekiel 43:25

Wewe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 43:18.

itakuwa kusu hilo

Hili neno limetumika ha hapa kuonyesha sehemu muhimu ya maelekezo.

sadaka zako za kuteketeza ... sadaka za amani ... kukupokea

Neno "yako" na "wewe" ni nafsi ya pili umoja inarejea kwa watu wa Israeli kwa ujumla.

nitakupokea

"nitakupokea kwa fadhila" au "nitafurahishwa na wewe"

Ezekiel 44

Ezekiel 44:1

iliyoelekea mashariki

Tazama jinsi ilivyotafsiriwa katika sura 40:5.

haitafunguliwa

"hakuna mtu atakaye ufungua"

Mungu wa Israeli

Tazama jinsi ilivyo tafsiriwa katika sura ya 8:3.

varanda

Tazama tafsiri yake katika 8:16.

mbele ya Yahwe

"mbele ya Yahwe" au "katika uwepo wa Yahwe"

Ezekiel 44:4

Kisha aka

"Kisha yule mtu" au "Kisha Yahwe"

tazama

Neno "tazama" hapa inaonyesha kwamba Ezekieli alishangazwa kwa kile alichokiona.

neno la Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 3:12.

nikaanguka kifudi fudi

Tazama tafsiri yake katika sura ya 1:27.

weka moyo wako

Tazama tafsiri yake katika sura ya 40:3.

taratifu zake zote

"maelekezo yote kuhusu nyumba ya Yahwe"

Ezekiel 44:6

Acheni matendo yenu maovu yatoshe kwa ajili yenu

"Matendo yenu maovu yamezidi kwa ajili yenu"

matendo maovu

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:9.

Ezekiel 44:8

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa watu wa Israeli.

Ezekiel 44:10

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa nyumba ya Israeli.

ni watumishi katika patakatifu pangu

"watakuwa watumishi katika hekalu langu"

kutazama malango ya nyumba

"kufanya kazi ya ulinzi kwenye malango ya nyumba"

watasimama mbele ya watu na kuwaokoa

"hawa Walawi watasimama mbele ya watu, ili kwamba waweze kuwaokoa watu"

nitainua mkono wangu kuapa kiapo

"nimeinua mkono wangu kuapa kiapo"

Ezekiel 44:13

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia ezekieli ujumbe kwa nyumba ya Israeli.

Wao

"Hawa Walawi"

Watakuja karibu

Tazama tafsiri yake katika sura ya 40:46.

watabeba lawama zao na hatia

"wataaibika na kuteseka matokeo"

matendo ya machukizo

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:9.

watunzaji

mtu ambaye kazi yake ni kulinda au kuangalia kitu au mtu

kitakacho fanyika ndani yake

"kwamba wanataka kufanya ndani yake."

Ezekiel 44:15

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekili ujumbe wake kwa Israeli.

hao wana wa Zadoki waliokamilisha

"ambao ni uzao wa Zadoki na kukamilisha"

walipokuwa mbali nami

Hili neno linamaanisha "kuacha kumsikiliza na kunitii."

watakuja karibu nami

"watanikaribia"

hili ndilo tangazo la Bwana Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:11.

Ezekiel 44:17

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa nyumba ya Israeli kuhusu uzao wa Zadoki wanao tumika kama makuhani.

Kwa hiyo itakuwa hivyo

"Kwa hiyo"

ua wa ndani

Tazama tafsiri yake katika sura ya 8:16.

kitani

Tazama tafsiri yake katika sura ya 9:1.

sufu

ngua iliyotengenezwa kwa nywele laini za kondaa

vilemba

Kilemba ni kitu kinachofunika kichwani ambacho kimetengenezwa na nguo ndefu kuzunguka kichwa.

Ezekiel 44:19

Maelezo ya Jumala:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa nyumba ya Israeli kuhusu uzao wa Zadoki unaotumika kama makuhani.

ua wa nje

tazama tafsiri yake katika sura ya 10:3.

Ezekiel 44:20

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa nyumba ya Israeli kuhusu uzao wa Zadoki ambao ulitumika kama makuhani.

nyoa

kata nywele za mtu kuwa fupi ili iwezekane kuona ngozi ya kichwa

punguza nywele za vichwa vyao

"kata nywele juu ya vichwa ili ziweze kuwa ndefu au ndefu wala fupi"

mjane

mwanamke ambaye amefiwa na mume wake

kutoka kwenye mstari wa nyumba ya Israeli

"ambaye uzao wake ni watu wa Israeli"

nyumba ya Israeli

Tazama tafsiri yake katika sura ya 3:1

Ezekiel 44:23

Maelezo ya Jumala:

Yahwe anaendela kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa nyumba ya Israeli kuhusu uzao wa Zadoki ambaye anatumika kama makuhani.

mjadala

"majadiliano"

Ezekiel 44:25

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa nyumba ya Israeli kuhusu uzao wa Zadoki ambao ulitumika kama makuhani.

hili ni tangazo la Bwana Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:11.

Ezekiel 44:28

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa nyumba ya Israeli kuhusu uzao wa Zadoki ambaye hutumika kama makuhani.

na ninyi

Hili neno "ninyi" linarejea kwa watu wa Israeli.

mali

nchi ambayo mtu humiliki na hutumia kuandaa kwa ajili ya mahitaji ya familia yake

katika Israeli

"katika nchi ya Israeli"

Ezekiel 44:30

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa nyumba ya Israeli kuhusu uzao wa Zadoki ambaye hutumika kama makuhani.

malimbuko

Hapa "malimbuko" huenda inamaanisha kwamba vitu bora miongoni mwa sadaka zote zilizowekwa karibu kumtolea Mungu.

na kila kitu kitokanacho na sadaka

"na kila zawadi ya kitu chochote kutoka zawadi zako zote"

ili kwamba baraka iweze kukaa katika nyumba zenu

Hili neno linamaanisha "hivyo nitabariki familia yako na kila kitu ambacho ni mali yako."

au mnyama aliyeraruliwa, iwe ni ndege au mnyama

"au kiumbe ambaye ni ndege au mnyama wa porini amerarua."

Ezekiel 45

Ezekiel 45:1

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa nyumba ya Israeli.

maeneo yote yanayoizunguka

"eneo lote ndani ya mipaka inayoizunguka"

Ezekiel 45:3

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaedelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa nyumba ya Israeli.

hili eneo

hekalu na mpaka unaoizunguka

fungu

"fungu la nchi"

dhiraa

Tazama jinsi ilivyotafsiriwa katika sura ya 40:5.

Ezekiel 45:6

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa nyumba ya Israeli.

imewekwa akiba kwa ajili ya mahali patakatifu

"ambayo uliyoitoa kwa ajili ya mahali patakatifu."

Urefu utalingana na urefu wa moja ya hayo mafungu

Inaonyesha kwamba Ezekieli analinganisha nchi ya mwana mfalme na ukubwa wa nchi iliyotolewa kwa kila makabila.

kutoka magharibi hata mashariki

Inaonyesha kwamba hii ilikuwa mipaka ya magharibi na mashariki mwa nchi ya Israeli.

Ezekiel 45:8

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaedelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa nyumba ya Israeli

Hii nchi itakuwa mali ya mwana mfalme katika Isaraeli

"Katika nchi, hii itakuwa mali ya mwana mfalme miongoni mwa watu wa Israeli"

Ezekiel 45:9

Inatosha kwa ajili yako

"Umefanya mengi kwa ajili ya hii"

vipimo

ni kifaa ambacho kilichokuwa kikitumika kupimia vitu ambavyo watu walivyovinunua au kuuza

ili kwamba birika liwe la homeri

"ili kwamba mabirika yatakuwa kiasi sawa kama homeri"

homeri

kama lita 220

shekeli

kama gram 11

gera

kama gram 0.55

mane

kama gram 660

Ezekiel 45:13

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa wana mfalme wa Israeli.

kwa kila homeri ya ngano

Inaonyesha kwamba hiki kiasi cha ngano ambacho watu huvuna. "kwa kila homeri ya ngano kutoka mavuno."

Maelekezo ya sadaka ya mafuta itakuwa

"Hii ni kanuni kuhusu mafuta, kuhusu birika la mafuta

mwagilia mikoa ya Israeli

"sehemu za Israeli zinazopata kiasi kizuri cha maji"

itatumika

"Utatumia hii migawanyiko kwa ajili"

Ezekiel 45:16

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa wana mfalme wa Israeli.

sikukuu za kudumu

"sikukuu zilizotengwa"

nyumba ya Israeli

Tazama tafsiri yake katika sura ya 3:1.

Ezekiel 45:18

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia ezekieli ujumbe wake kwa wana mfalme wa Israeli.

Katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi

Huu ni mwezi wa kalenda ya Kiebrania.

utachukua

Neno "uta" ni umoja na linarejea kwa yeyote aliye mwana mfalme katika Israeli.

katika saba ya mwezi

"siku ya saba ya mwezi wa kwanza"

kwa dhambi ya mtu yeyote kwa ajali

"kwa kila mtu aliyefanya dhambi bila kukusudia"

au upuuzi

"au aliasi kwa sababu hakujua vyema"

Ezekiel 45:21

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa wana mfalme wa Israeli.

Katika siku ya mwezi siku ya kumi na nne ya mwezi

Huu ni mwezi wa kalenda ya Kiebrani.

kwa ajili yanu

Neno "yenu" ni wingi na inarejea kwa mwana mfalme na watu wengine wa nyumba ya Israeli.

Ezekiel 45:23

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa wana mfalme wa Israeli.

sadaka ya chakula

Hii pia inaitwa "sadaka ya unga."

ng'ombe dume saba na kondoo dume saba wasio na dosari

ng'ombe dume na kondoo dume ambao wana afya kabisa"

efa

"lita ishirini na mbili"

hini

"lita ishirini na moja"

Ezekiel 45:25

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia ezekieli ujumbe wake kwa wana mfalme wa Israeli.

Katika mwezi wa saba siku ya kumi na tano ya mwezi

Huu ni mwezi wa kalenda yaKiebrania.

kwenye sikukuu

Hii ni sikukuu tofauti kuliko sikukuu ambayo Ezekieli alikuwa akiielezea kabla.

Ezekiel 46

Ezekiel 46:1

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa wana mfalme wa Israeli.

ua wa ndani

Tazama tafsiri yakekatika sura ya 8:16.

kuelekea mashariki

Tazama tafsiri yake katika sura ya 11:1.

lango la ndani

Tazama jinsi ilivyo tafsiriwa katika sura ya 40:17

Ezekiel 46:3

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa wana mfalme wa Israeli.

mbele ya Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 43:22.

Ezekiel 46:6

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia ezekieli ujumbe wake kwa wana mfalme wa Israeli.

varanda

Tazama jinsi ilivyo tafsiriwa katika sura ya 40:8.

Ezekiel 46:9

mbele ya Yahwe

Tazama jinsi ilivyo tafsiriwa katika sura ya 44:1

sikukuu zilizoteuliwa

Tazama tafsiri yake katika sura ya 36:37.

Ezekiel 46:11

kwa ajili ya hiyo

"kwa ajili yake"

Ezekiel 46:13

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia ezekieli ujumbe wake kwa wana mfalme wa Israeli.

kutia maji kidogo

"ambayo italowa"

Ezekiel 46:16

mwaka wa uhuru

Huu ni mwaka ambao mtumishi alipata uhuru. Huu pia unaitwa "Mwaka wa Jubilii."

Ezekiel 46:19

ambao ulielekea kaskazini

"ambao ulikuwa malango yao makuu kuelekea kaskazini"

Tazama!

Neno "tazama" hapa linaonyesha kwamba Ezekieli aliona kitu kinacho vutia.

ua wa nje

Tazama jinsi ilivyo tafsiriwa katika sura ya 10:3.

Ezekiel 46:21

ua wa ndani

Tazama tafsiri yake katika sura ya 10:3.

Ezekiel 47

Ezekiel 47:1

kuelekea mashariki

Tazama jinsi ilivyo tafsiriwa katika sura ya 40:5.

hata kulia kwa madhabahu

Huu ni upande wa kulia wa madhabahu wakati mtu alionekana katika huo wakati walipoelekea mashariki.

Ezekiel 47:3

kipimo cha mstari

ni gidamu au kamba ambayo watu hutumia kupimia umbali mrefu

Ezekiel 47:6

Mwanadamu

Tazama tafsiri yake katika sura ya 2:1.

unaona hii

"Kuwa makini na hii"

Ezekiel 47:9

Kisha itakuwa

Tazama tafsiri yake katika sura ya 21:6.

En Gedi

ni chemichemi mkubwa upande wa magharibi mwa Bahari ya Chumvi

kukausha

"kwa ajili ya watu kukausha"

En Eglaimu

ni chemichemi kubwa upande wa magharibi mwa Bahari ya Chumvi

Ezekiel 47:11

tapakaa maji

maeneo ambayo yenye maji lakini pia tope

mabwawa

mahali ambapo kuna kina kifupi cha maji

Ezekiel 47:13

Yusufu atakuwa na mafungu mawili

"uzao wa Yusufu utapokea maeneo mawili ya nchi."

kila mtu na ndugu miongoni mwenu

Hili neno linamaanisha "kila mtu apokee kiasi cha nchi sawa

nimeinua mkono wangu kuapa

Tazama jinsi ilivyo tafsiriwa katika sura ya 20:4.

katika njia moja

"hivyo, hasa, hii"

Ezekiel 47:15

Hethloni

ni jina la mahali ambapo palikuwa na njia ndogo za kaskazini na mashariki mwa Tripoli.

Zadadi

ni jina la mji katika Lebanoni ambao ulikuwa katika sehemu moja ambayo ni Sadai kwa sasa.

Barota

ni sehemu katika Lebanoni ambayo ipo kusini kidogo mwa Baalbeki ilipo

Sabraimu

ni sehemu kati ya Damskasi na Hamathi

Hazeri Hatokoni

ni sehemu ilikuwa karibu na kati ya Damaskasi na Haurani

Haurani

Hii ni sehemu ya mashariki mwa Bahari ya Galilaya.

Hazari Enoni

ni sehemu katika Siria.

Ezekiel 47:18

Tamari

ni mji kama kilomita thelathi ni mbili kusini magharibi kutoka sehemu ya kusini ya Bahari ya Chunvi

Meriba Kadeshi

ni sehemu ya mpaka kati ya Israeli na Misri, nusu ya njia kati ya Bahari ya Shamu na Bahari ya Mediteria

kijito cha Misri

ni bonde kubwa sana katika sehemu ya kaskazi mwa Sinai

Ezekiel 47:21

kwa ajili yenu wenyewe

Neno "yenu wenyewe" ni wingi na linarejea kwa watu wa Israeli.

Kisha itakuwa kwamba

Tazama jinsi ilivyo tafsiriwa katika sura ya 21:6.

hili ndilo tangazo la Bwana Yahwe

Tazama jinsi livyo tafsiriwa katika sura ya 5:11.

Ezekiel 48

Ezekiel 48:1

fungu moja la nchi

"kipande kimoja cha nchi ambacho utakigawanya"

Hethloni ... Lebo ... Hazari Enani

Tazama jinsi ilivyo tafsiriwa katika sura ya 47:15.

Ezekiel 48:4

fungu moja

"fungu moja la nchi"

kunyoosha kutoka upande wa mashariki kwenda upande wa magharibi

Tazama jinsi ilivyo tafsiriwa katika sura ya 48:1.

Ezekiel 48:8

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekile ujumbe wake kwa watu wa Israeli

dhiraa

"urefu"

upana

"kutoka kaskazini hata kusini"

Ezekiel 48:10

Sadaka kwa ajili yao itakuwa fungu la hii nchi takatifu sana

"Hili fungu dogo ndani ya fungu takatifu la nchi litamilikiwa na hawa makuhani, fungu ambalo ni takatifu zaidi kuliko yote ya fungu takatifu la nchi"

Ezekiel 48:13

haya malimbuko

"hii nchi ni malimbuko." Hapa "malimbuko" huenda inamaanisha vitu bora miongoni mwa sadaka zote zilizowekwa pembeni kumtolea Mungu.

Ezekiel 48:15

itakuwa kwa wote wanayoitumia hiyo nchi

"itakuwa nchi ambayo imeungana na watu wa mji"

nyumba, na mahali pa malisho

"mahali kwa ajili ya nyumba na kwa ajili ya sehemu za wazi"

Ezekiel 48:17

uzalishaji wake

"vitu vinavyomea huko"

Ezekiel 48:19

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa watu wa Israeli.

Kwa njia hii mtatengeneza matoleo matakatifu ya nchi, pamoja na nchi kwa ajili mji

"Utatoa sadaka takatifu na pia mali ya mji"

ninyi

Huu wingi unarejea kwa watu wa Israeli.

sadaka takatifu

nchi ambayo watu wa Israeli waliyopewa na Yahwe kwa ajili ya Walawi, makuhani, na hekalu

Ezekiel 48:21

sadaka takatifu

Tazama jinsi ilivyotafsiriwa katika sura ya 48:17.

Ezekiel 48:23

fungu moja

Tazama jinsi ilivyo tafsiriwa katika sura ya 48:1, "fungu moja la nchi"

Ezekiel 48:27

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kumpatia Ezekieli ujumbe wake kwa watu wa Israeli.

Tamari ... Meriba Kadeshi ... kitabu cha Misri

Tazama tafsiri yake katika sura ya 47:18.

ninyi

Huu wingi unarejea kwa watu wa Israeli.

Hili ndilo tangazo la Yahwe

Tazama tafsiri yake katika sura ya 5:11.

Ezekiel 48:30

dhiraa

Tazama tafsiri yake katika sura ya 40:5.

dhiraa 4,500

kama kilomita 2.4

Ezekiel 48:33

dhiraa

Tazama tafsiri yake katika sura ya 40:5.

dhiraa

kama kilomita 2.4

Daniel 1

Daniel 1:1

Nebukadneza

Jina hili humrejelea Nebukadneza na wanajeshi wake, siyo yeye peke yake.

kuzuia mahitaji yake yote

"Kuwazuia watu wasipokee mahitaji"

Yehoyakimu mfalme wa Yuda

Hii inamrejelea Yehoyakimu na wanajeshi wake, siyo Yehoyakimu peke yake.

alimpatia

Yehoyakimu alimpa Nebukadneza

alivipeleka ...aliviweka

Ingawa Nebukadneza hakufanya vitu hivi peke yake, ni vizuri kwa msomaji kutumia umoja tu.

Alivipeleka

Kiwakilishi 'vi' kinarejelea vitu/vifaa vitakatifu vilivyochukuliwa kutoka Yerusalemu.

hazina ya mungu wake

Hiki kitendo kilikuwa na ibada kwa mungu wake

Daniel 1:3

mfalme akamwambia

inmrejelea Nebukadneza

Ashipenazi

Huyu alikuwa na afisa wake mkuu

kiungwana

hili ni tabaka la juu sana la kijamii

wasio na hila

Maneno haya mawili ya kukanusha kwa pamoja yametumika kutilia mkazo wazo chanya. "wenye mwonekano kamili"

wenye kujawa na ufahamu na weledi

Hii ni nahau. Hii ina maana ya kwamba walijua vitu vingi na waliweza kupanga na kutumia maelezo yale.

ikulu ya mfalme

Hii ni nyumba au jengo kubwa mahali ambapo mfalme aliishi

Alitakiwa kuwafundisha

"Ashipanezi alitakiwa kuwafundisha"

Mfalme aliwatengea kwa ajili yao

Maafisa wa mfalme walifanya hivyo kwa niaba ya mfalme.

chakula kizuri

Chakula maalumu, adimu na kizuri ambacho mfalme alikula.

Vijana hawa walitakiwa kufunzwa

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Ashipenazi alitakiwa kuwafunza vijana hawa"

kufunzwa

"kufundisha maarifa"

Daniel 1:6

miongoni mwao

Miongoni mwa vijana kutoka Israeli

Afisa mkuu

Inamrejelea Ashipenazi aliyekuwa afisa wa juu sana katika utawala wa Mfalme Nebukadneza.

Belteshaza...Shadraka...Meshaki...Abednego

Haya yote ni majina ya wanaume.

Daniel 1:8

Danieli alinuia katika akili yake

Hapa neno "akili" linamrejelea Danieli mwenyewe. "Danieli aliamua mwenyewe"

asingejitia ujanisi

"kujitia unajisi" ni kukifanya kitu fulani kuwa kichafu. Baadhi ya vyakula na vinywaji vya Kibabeli vingemfanya Danieli kuwa mchafu kutokana na sheria za Mungu.

chakula kizuri

Hii inarejelea chakula maalumu,adimu na kizuri ambacho mfalme alikula.

Kwa nini awaone ninyi mkiwa mnaonekana vibaya kuliko vijana wengine wa umri wenu?

Afisa allitumia swali hili ili kuelezea kile alichodhani kuwa kingetokea. Pia yaweza kuwa maelezo kama "Hataki kuwaoneni ninyi mkionekana kuwa wabaya zaidi ya vijana wengine wa umri wenu"

Mfalme aweza kukitwaa kichwa changu

Hii ni nahau "Mfalme aweza kukikata kichwa changu" au "Mfalme aweza kuniua"

Daniel 1:11

ulinganishe mwonekano wetu na mwonekano

Danieli alimwomba msimamizi kuangalia kama yeye na rafiki zake walionekana vibaya kuliko vijana wengine.

Daniel 1:14

aliwajaribu...mwonekano wao...ulikuwa...vyakula ..na vinywaji vyao

Viwakilishi hivi vyote vinawarejelea akina Danieli, Hanania, Mishaeli na Azaria.

wenye afya

Hii ina maana kwamba walikuwa wenye afya nzuri kutokana na kile walichokula.

Daniel 1:17

Mungu aliwapa uelewa na ufahamu

Hii inaweza kuongezwa ili kwamba nomino dhahania "Uelewa na ufahamu" zaweza kuelezwa kwa kutumia vitenzi "kujifunza na kufahamu" yaani "Mungu aliwapa uwezo wa kujifunza na kufahamu kwa uwazi"

maandiko yote na hekima

Haya ni maneno ya kutia chumvi kuonesha kwamba walikuwa na elimu na ufahamu mzuri

Daniel 1:19

Mfalme aliongea nao

Mfalme aliongea na vijana wanne (1:17)

miongoni mwa kundi lote hapo hapakuwa na wa kuwalinganisha na akina Danieli,Hanania, Mishaeli, na Azaria

Hii yaweza kuelezwa kwa kutumia muundo kubalifu. "Danieli, Hanania, Mishaeli na Azaria walimfurahisha sana zaidi ya mtu yoyote katika kundi"

"Danieli, Hanania, Mishaeli na Azaria

Haya ni majina ya wanaume.

mara kumi zaidi

hapa maneno "mara kumi" yanatia chumvi kumaanisha ubora wa hali.

kwanza wa Mfalme Koreshi

"mwaka wa kwanza wa mfalme Koreshi alitawala Babeli."

Daniel 2

Daniel 2:1

katika mwaka wa pili

"ndani ya mwaka wa pili"

alikuwa na ndoto

"Nebukadneza aliota ndoto"

akili yake ilisumbuka

Hapa neno "akili" linarejelea mawazo yake. "mawazo yake yalimsumbua"

na hakuweza kulala

Mawazo yake yaliyomsumbua yalimzuia asipate usingizi.

Ndipo mfalme alipowaita waganga

"kisha mfalme aliwaita waganga"

wafu

"watu waliokwisha kufa"

walikuja

"waliingia ndani ya ikulu"

walisimama mbele

"walisimama mbele ya "

Daniel 2:3

akili yangu ina mashaka

hapa neno "akili" linamrejelea mfalme mwenyewe.

mashaka

"kusumbuka"

Kiaramaiki

Hii ni lugha ambayo watu wa Babeli waliiongea.

" Mfalme, aishi milele!

Watu waliyasema maneno haya kuonesha heshima kwa mfalme. "Mfalme, tunatumaini utaishi milele"

sisi, watumishi wako

Watu walijiita wao wenyewe kuwa ni watumishi wa mfalme kuonesha heshima.

tutaifunua

Hapa kiwakilishi 'tu' kinarejelea watu/wanaume ambao mfalme alikuwa akiongea nao na hakimjumuishi mfalme.

Daniel 2:5

Jambo hili limeshamalizika

Maneno haya yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Nimeamua cha kufanya juu ya jambo hili"

miili yenu itakatwa vipande vipande na nyumba zenu zitafanywa kuwa vichuguu vya uchafu

Maneno haya yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Nitawaamuru wanajeshi wangu kukata miili yenu katika vipande na kuzifanya nyumba zenu kuwa vichuguu vya uchafu"

mtapokea zawadi kutoka kwangu

Maneno haya yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Nitawapeni zawadi"

Daniel 2:7

Mfalme na atuambie

Watu wenye hekima walimweleza mfalme kwa nafsi ya tatu kama ishara ya heshima.

mmeona maamuzi yangu ni magumu kuhusu jambo hili

Maamuzi ambayo hayatabadilika yanasemwa kama ni kitu ambacho ni imara. "mmeona kwamba sitabadili maamuzi yangu juu ya hili"

kuna sentensi moja tu kwa ajili yenu

"kuna hukumu moja kwa ajili yenu"

uongo na maneno ya kudanganya

Maneno haya mawili kwa ukaribu yanamaanisha kitu kile kile na kutia mkazo kwamba huu ni "uongo uliokusudia kudanganya."

Daniel 2:10

mkuu na mwenye nguvu

Maneno haya mawili kimsingi yanamaanisha kitu kile kile na kutia mkazo juu ya ukubwa wa nguvu za Mfalme.

hakuna yeyote awezaye kumwambia mfalme isipokuwa miungu

Maneno haya hameelezwa kwa kukanusha kwa ajili ya kutia mkazo. Yaweza pia kuelezwa kwa sentensi chanya. "Ni miungu tu yaweza kumwambia mfalme hili"

Daniel 2:12

kasirike na kughadhabika

Maneno haya kimsingi yanamaanisha kitu kile kile na kutia mkazo juu ukali wa hasira yake.

wale wote katika Babeli

"watu wote katika Babeli"

Hivyo, amri ilitoka

Amri inaongelewa kama ni kitu chenye uhai na chenye uwezo wa kwenda nje. "Mfalme aliipitisha amri"

wale wote waliojulikana kwa hekima yao ni lazima wauawe

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Wanajeshi walitakiwa kuwaua watu wote waliojulikana kwa hekima zao"

ili kwamba wauawe

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "kwa lengo la kuwaua"

Daniel 2:14

busara na umakini

Maneno haya mawili kimsingi yanamaanisha kitu kile kile na kutia mkazo juu ya ukubwa wa busara.

Arioki

Hili ni jina la kamanda wa mfalme.

walinzi

Hili ni kundi la watu ambao kazi yaoni kumlinda mfalme

ambaye alikuwa amekuja kuwaua

ambaye mfalme alikuwa amemtuma ili kuua"

Danieli aliingia ndani

Huenda Danieli alienda katika ikulu. "Danieli alienda katika ikulu"

akaomba ahadi ya muda wa kuonana na mfalme

"aliomba muda maalumu uliopangwa ili kukutana na mfalme"

Daniel 2:17

nyumba yake

Hii inarejelea nyumba ya Danieli

kile kilichotokea

"kuhusu amri ya mfalme"

Aliwasihi kutafuta rehema

"Aliwaomba waombe huruma"

ili kwamba yeye na wao wasije wakauawa

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Ili kwamba mfalme asije akawaua"

Daniel 2:19

Usiku ule siri ilifunuliwa

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Usiku ule Mungu aliifunua siri"

siri

hii inarejelea ndoto ya mfalme na tafsiri yake.

"Litukuzwa jina la Mungu

Hapa"jina" linamrejelea Mungu mwenyewe. "Mungu atukuzwe"

Daniel 2:21

Maelezo ya jumla

Mistari hii pia ni sehemu ya sala ya Danieli.

anaondoa wafalme

"huyaondoa mamlaka ya kifalme ya kutawala"

kuweka wafalme katika viti vyao vya enzi

Kuwa katika kiti cha enzi ina maana ya kutawala ufalme. "huwafanya wafalme wapya kutawala juu ya falme zao."

naye anaishi pamoja na mwanga.

"Mwanga hutoka sehemu ambako Mungu aliko"

Daniel 2:23

Maelezo ya jumla

Mstari huu pia ni sehemu ya sala ya Danieli. Aliacha kumwongelea Mungu kwa nafsi ya tatu na alianza kutumia nafsi ya pili.

umeyafanya yawe wazi kwetu yale tuliyokuomba

"aliniambia marafiki zangu na nilikuomba utuambie."

umetujulisha mambo yamhusuyo mfalme

"alituambia kile ambacho mfalme alitaka kujua"

Daniel 2:24

Arioki

Hili ni jina la Kamanda wa Mfalme.

kila mtu aliyekuwa na hekima

"watu wenye hekima"

Daniel 2:25

Beliteshaza

Hili ni jina ambalo Wababeli walimpa Danieli.

Daniel 2:27

Siri ambayo mfalme ameiomba haiwezi kufunuliwa na watu wenye hekima, wala wale wenye kuongea na wafu, wala wachawi, na wala wataalamu wa nyota

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Wale wenye hekima, wale wenye kuongea na wafu, waganga na wanajimu hawawezi kufunua siri kuhusu kile mfalme alichokiomba"

Siri ambayo mfalme ameiomba

Kirai hiki knarejelea ndoto ya mfalme.

Daniel 2:29

Maelezo ya jumla

Danieli anaendelea kuongea na Mfalme

yule afichuaye siri

Kirai hiki kinamrejelea Mungu. "Mungu ambaye hufunua siri"

siri hii haikufunuliwa kwangu

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Mungu hakuifunua siri hii kwangu"

Siri hii imefunliwa kwangu ili kwamba wewe

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji.

Amefunua siri hii kwangu ili kwamba wewe

Kirai hiki kinatumia kiwakilishi "wewe" kumrejelea mtu katika akili.

Daniel 2:31

Maelezo ya jumla

Daniel anaendelea kuongea na mfalme

kilikuwa kimetengenezwa kwa dhahabu safi

"kilikuwa cha dhahabu safi" au "ilikuwa dhahabu nzuri"

sehemu chuma na sehemu kwa udongo

"ilikuwa kwa sehemu chuma na sehemu nyingine udongo"

Daniel 2:34

Maelezo ya jumla

Danieli anaendelea kuongea na mfalme.

jiwe lilikuwa limechongwa, ingawa si kwa mikono ya wanadamu, na lili...

Maneno haya yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji kama yatagawanywa katika sehemu mbili. "mtu fulani alilikata jiwe kutoka mlimani, lakini si mtu aliyelikata jiwe. Jiwe..."

kama makapi yaliyo katika sakafu za kupuria kipindi cha kiangazi

kirai hiki kinalinganisha vipande vya sanamu na vitu vidogo vilivyo vyepesi na ambavyo vinaweza kupeperushwa mbali na upepo. "kama vipande vikavu vya nyasi vinavyopeperushwa na upepo"

hakuna alama inayoachwa

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo chanya. "viliondolewa kabisa"

kuijaza dunia yote

"kuenea dunia yote"

Daniel 2:36

Maelezo ya jumla

Danieli anaendelea kuongea na mfalme

Na sasa tutamwambia mfalme

Hapa kiwakilishi "tu" kinamrejelea Danieli peke yake. Inawezekana ametumia muundo wa wingi katika unyenyekevu kuepuka kuchukua heshima kwa kujua maana ya ndoto ambayo Mungu ameifunua kwake.

mfalme wa wafalme

"mfalme wa muhimu sana" au "mfalme anayetawala juu ya wafalme wengine"

nguvu, uweza

Maneno haya kimsingi yanamaanisha kitu kile kile.

Amevitia mkononi mwako

Hapa neno "mkono'' linarejelea utawala. "amekupa utawala"

sehemu ambazo binadamu huishi

sehemu imetumika kuwakilisha watu ambao wanaishi hapo.

Amekupa wanyama wa mwituni na ndege wa angani katika mkono wako,

Hapa neno "mkono" linarejelea utawala. "Amekupa utawala juu ya wanyama wa mwituni na ndege wa angani"

ndege wa angani

hapa neno "angani" limetumika kumaanisha mbinguni.

Wewe u kichwa cha dhahabu cha sanamu

Katika ndoto ya mfalme kichwa cha sanamu kinamwakilisha mfalme. "Kichwa cha dhahabu kinakumaanisha wewe mfalme"

Daniel 2:39

Maelezo ya jumla

Danieli anaendelea kuongea na mfalme

ufalme mwingine utainuka

Katika ndoto ya mfalme ilionekana kwamba ufalme wake ni wa dhahabu, hivyo ufalme mdogo utakuwa wa shaba. "ufalme mwingine ambao ni shaba utainuka"

hata ufalme wa tatu wa shaba

"bado ufalme wa tatu ambao ni wa shaba" au kisha bado kuna ufalme mwingine ambao unawakilishwa na shaba katika sehemu ya sanamu"

Daniel 2:40

Maelezo ya jumla

Danieli anaendelea kuongea na mfalme

kutakuwa na ufalme wa nne

"kutakuwa na ufalme wa namba ya nne''

wenye nguvu kama chuma

Ufalme wa nne unaongelewa kuwa na nguvu kama chuma

Itaviharibu vitu hivi vyote na kuvisaga.

Lugha hii mfano inamaana ya kwamba ufalme wa nne utashinda na kuchukua nafasi ya falme zingine.

vitu hivi vyote

"falme zilizopita/zilizotangulia"

Daniel 2:41

Maelezo ya jumla

Danieli anaendelea kuongea na mfalme

kama vile ulivyoona

Nebukadneza alione miguu iliyo na udongo na chuma. Hakuweza kuona mchakato wa utengenezaji wa miguu.

vilikuwa kwa sehemu vimetengenezwa kwa udongo na kwa sehemu vimefanywa kwa chuma,

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "ilikuwa ya mchanganyiko wa udongo na chuma"

hawatakaa kwa pamoja

"hawatabaki wameshikamana"

Daniel 2:44

Maelezo ya jumla

Danieli anaendelea kuongea na mfalme

katika siku za wafalme hao

Katika kifungu hiki maneno "wafalme hao" yanawarejelea watawala wa falme zinazooneshwa katika sehemu mbalimbali za sanamu

ambao hautaweza kuangushwa, wala kushindwa na watu wengine

Maneno haya yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. " kwamba hakuna hata mmoja ambaya ataangamizwa, na ya kwamba watu wengine hawatashinda."

jiwe lilichongwa kutoka katika mlima, lakini si kwa mikono ya wanadamu

Maneno haya yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "mtu fulani alilikata jiwa kutoka mlimani, lakini si mtu aliyelikata"

kuaminika

aminifu na sahihi

Daniel 2:46

alianguka kifudifudi

Tendo hili linaonesha kwamba mfalme alikuwa anamheshimu Danieli. "lala chini huku kichwa kimeelekea chini."

sadaka zitolewe na manukato yatolewe kwake

Maneno haya yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Watumishi wake walitoa sadaka na kutoa manukato kwa Danieli."

Hakika Mungu wako

"Ni kweli kwamba Mungu wako"

Mungu wa miungu, Bwana wa wafalme,

"mkuu kuliko miungu mingine, na mfalme juu ya wafalme wengine wote"

ambaye hufunua mafumbo

"yeye ambaye hufunua siri"

kufumbua mafumbo haya

"kufunua siri za ndoto yangu"

Daniel 2:48

Alimfanya kuwa mtawala

"Mfalme alimfanya Danieli kuwa mtawala"

Shadraka...Meshaki....Abeddinego

Haya yalikuwa ni majina ya Kibabeli waliyopewa vijana watatu wa Kiyahudi walikuwa wameletwa Babeli pamoja na Danieli.

Daniel 3

Daniel 3:1

urefu wa dhiraa sitini na upana dhiraa sita.

"urefu wa takribani mita 27 na upana upatao mita tatu"

uwanda wa Dura

Hii ni sehemu ndani ya ufalme wa Babeli.

magavana wote wa majimbo, magavana wa mikoa, na magavana wa vijiji

Haya ni madaraja ya mamlaka juu ya himaya ya ukubwa fulani.

wahazini

hawa ni maafisa walikuwa wanawajibika kwa mambo ya fedha

sanamu aliyokuwa ameiweka

hii inamhusu Mfalme Nebukadneza ambaye aliweka sanamu iliyojengwa kana kwamba alijijenga mwenyewe. "Sanamu ambayo Nebukadneza aliwaagiza watu wake kuiweka."

Daniel 3:3

magavana wa majimbo, magavana wa mikoa, na magavana

Angalia ulivyotafsiri katika 3:1

sanamu ambayo Nebukadneza aliyokuwa ameiweka

hii inamhusu Mfalme Nebukadneza ambaye aliweka sanamu iliyojengwa kana kwamba alijijenga mwenyewe. "Sanamu ambayo Nebukadneza aliwaagiza watu wake kuiweka."

mtangazaji

Huyu mtu ni mjumbe maalumu wa mfalme

mmeamriwa

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Mfalme anawaagizeni ninyi"

zeze

Hivi ni vyombo vya muziki ambavyo ni sawa na vinubi. Muundo wake ni wa pembe tatu na vina nyuzi nne.

kuanguka na kuisujudia ninyi wenyewe

Haya ni matendo ya alama ya kuabudu.

Daniel 3:6

Na yeyote asiyeanguka na kuiabuda, kwa wakati huo huo atatupwa katika tanuru la moto

Sentensi hii yaweza kuandikwa kwa muundo tendaji. " Wanajeshi watamtupa katika tanuru liwakalo moto mtu yeyote ambaye hataanguka na kuabudu sanamu katika muda ule watakaposikia muziki."

kuanguka

Hili ni tendo linaloonesha alama ya kuabudu.

tunuru liwakalo moto

Hiki ni chumba kikubwa kilicho jazwa moto

watu wote, mataifa na lugha

Maneno haya yanajumuisha kundi kubwa la maafisa kutoka katika miko mbalimbali waliokuwapo hapo.

sauti za pembe, filimbi, ala za muziki, zeze, vinubi na zumari na aina zote za muziki,

Hivi ni vyombo vya muziki.

walianguka na kuisujudia wao wenyewe

Haya ni matendo yanayoonesha ibada.

sanamu ya dhahabu ambayo Nebukadneza mfalme alikuwa ameiweka.

Hii inaongelea juu ya Mfalme Nebukadneza kutoa agizo kwamba ijengwe sanamu kana kwamba aliijenga mwenyewe. "Sanamu ya dhahabu ambayo Mfalme Nebukadneza aliwaagizawatu wake waiweke."

Daniel 3:8

mfalme aishi milele

Hii ilikuwa na salamu ya kawaida kwa mfalme

auti ya pembe, filimbi, ala za muziki, zeze, vinubi na zumari, na aina zote za muziki,

Angalia ulivyotafsiri orodha hii katika 3:3

kuanguka na kuisujudia sanamu ya dhahabu.

Haya ni matendo ya kuabudu.

Daniel 3:11

Mtu yeyote asiyeanguka na kuiabudu sharti atupwe katika tanuru linalowaka moto

Tungo hii yaweza kuelezwa kwa kutumia muundo tendaji. "Wanajeshi watawatupa katika tanuru liwakalo moto mtu yeyote ambaye hatalala chini na kuabudu."

kuanguka chini

Hili ni tendo la ishara ya kuabudu

tanuru la moto

Hiki ni chumba kikubwa chenye moto mkali

masuala

"mambo" au "shughuli"

Shadraka, Meshaki, na Abednego

Haya yalikuwa ni majina ya Kibabeli ya vijana watau wa Kiyahudi ambao walikuwa ni marafiki wa Danieli.

hawakutii wewe

"hawakusikilizi wewe"

kuisujudia wenyewe

Hii ni ishara ya tendo la kuabudu

sanamu ya dhahabu ambayo umeiweka

Hii inazungumzia juu ya mfalme Nebukadneza kutoa amri ya kujengwa kwa sanamu kana kwamba yeye mwenyewe aliijenga. "Sanamu uliyowaagiza watu wako waijenge"

Daniel 3:13

alijawa na hasira na ghadhabu

Hasiria na ghadhabu ya mfalme Nebukadneza ilikuwa ni kubwa na ya kwamba inaongelewa kana kwamba ilikuwa imemjaa. Mahali hapa maneno "hasira na ghadhabu" yanamaanisha kitu kile kile na yametumika kuonesha mkao juu ya vile mfalme alivyokasirishwa.

Shadraka, Meshaki na Abednego

Haya ni majina ya Kibabeli ya marafiki watatu wa Kiyahudi wa Danieli.

Je mmejipanga katika akili zenu

hapa neno "akili" linarejelea juu ya kufanya maamuzi. Ni nahau yenye maana ya kuamua kwa dhati.

kuisujudia wenyewe

Hili ni tendo la ishara ya kuabudu.

sanamu ile ya dhahabu ambayo nimeiweka

Hii inazungumzia juu ya mfalme Nebukadneza kutoa amri ya kujengwa kwa sanamu kana kwamba yeye mwenyewe aliijenga. "Sanamu uliyowaagiza watu wako waijenge"

Daniel 3:15

sauti pembe, filimbi, ala za muziki, zeze, vinumbi na zumari, aina zote za muziki

Hivi ni vyombo au ala za Muziki

kuanguka chini na kuisujudia wenyewe

Haya ni matendo yanayoashiria ibada.

mambo yote yatakuwa mazuri

"hapatakuwa na shida zaidi' au "mtakuwa huru kwenda"

sanamu ile ambayo nimeitengeneza,

Hii inazungumzia juu ya mfalme Nebukadneza kutoa amri ya kujengwa kwa sanamu kana kwamba yeye mwenyewe aliijenga. "Sanamu uliyowaagiza watu wako waijenge"

mtatupwa mara katika tanuru la moto

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "wanajeshi wangu

mtatupwa mara katika tanuru la moto

hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "wanajeshi wangu watawatupeni ninyi katika moto uwakao."

tanuru la moto

Hiki ni chumba kikubwa chenye moto

Ni mungu gani.... katika mikono yangu?"

Mfalme hatarajii jibu. Anawatisha vijana watatu. "Hakuna mungu awezaye kuwaokoeni katika nguvu zangu"

kutoka katika mikono yangu

Mahali hapa neno "mikono" lina maana ya nguvu, mamlaka ya kuhukumu.

Daniel 3:16

Nebukadneza, hatuhitaji

Katika sehemu hii watu watatu wanaongea na Mfalme bila kutumia wadhifa wake. Hii ni hali ya kuonesha dharau kwa mamlaka yao.

Kama sivyo, na ijulikane kwako, wewe mfalme,

"Lakini mfalme unapaswa kujua kwamba hata kama Mungu wetu hatatuokoa sisi"

sanamu ya dhahabu uliyoiweka.

Katika kirai hiki, kiwakilishi "u" hakimhusu mfalme kuiweka sanamu, bali mfalme aliamuru watu wake waisimamishe.

Daniel 3:19

Nebukadneza alijawa na ghadhabu

Mfalme alikuwa amekasirika kwa kiwango kwamba hasira yake inasemwa kana kwamba ilikuwa imemjaa.

Daniel 3:21

kilemba

Kilemba ni kipande cha nguo kinachovaliwa ili kufunika kichwa.

Kwasababu ya agizo la mfalme lilifuatwa

Maneno haya yweza kuandikwa kwa muundo tendaji. "Kwasababu watu walilifuata agizo la mfalme kwa usahihi."

Daniel 3:24

Je hatukutupa watu watatu wakiwa wamefungwa katika moto?

"Tuliwatupa watu watatu katika moto wakiwa wamefungwa, sawa?"

Mng'ao wa mtu wa nne ni kama

"Mtu wa nne anatao mng'ao mkali"

kama mwana wa miungu."

miungu iliaminika kuwa ilikuwa iking'aa sana kwa mwanga. "Mtu wa nne anang'aa sana kama ing'aavyo miungu."

Daniel 3:26

Magavana wa majimbo, magavana wengine

Haya ni madaraja ya mamlaka juu ya himaya tofauti tofauti.

nywele katika vichwa vyao hazikuungua

Muundo tendaji waweza kutumika kwa tungo hii."moto haukuweza kuunguza nywele vichwani mwao."

Kuungua

"kuchomeka"

mavazi yao yalikuwa hayajaharibiwa

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Moto haukuweza kuharibu mavazi yao."

na hawakuwa na harufu ya moto

"hawakunukia harufu ya moto"

Daniel 3:28

walipoikana amri yangu

Kutokutii amri ya mfalme kunasemwa kana kwamba kilikuwa kitendo dhahiri cha kutoka na kwenda mbali.

waliitoa miili yao

Kirai hiki kinawahusu watu watatu waliokuwa wamehialika kufa kwa kile wanachokiamini.

kusujudia

Kitendo hiki kina maana ya kulala katika nchi, uso ukiwa umeelekea chini, katika hali ya kuabudu.

isipokuwa Mungu wao

kwa mungu mwingine isipokuwa Mungu"

Daniel 3:29

watu wote, taifa au lugha ambayo itazungumza kitu chochote kinyume na Mungu wa Shadraka, Meshaki na Abedinego lazima wakatwe vipande, na ya kwamba nyumba zao lazima zifanywe kuwa vichuguu vya uchafu

Maneno haya yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "watumishi wangu watawaharibu watu wowote, taifa, au lugha... na kuzifanya nyumba zao kuwa vichuguu vya uchafu."

itazungumza kitu chochote kinyume na Mungu

"kuongea maneno ambayo yamheshimu Mungu"

lazima wakatwe vipande

"kukatwa kwa miili yao katika vipande

hakuna mungu mwingine anayeweza kuokoa kama hivi

Muundo wa kubalifu waweza kutumika hapa. "Ni Mungu wao tu aweza kuwaokoa kama hivi"

Daniel 4

Daniel 4:1

Maelezo ya jumla

Katika surahii, Nebukadneza anasema kile ambacho Mungu alimfanyia. Katika mistari ya 1-18, Nebukadneza anaeleza ndoto yake kwa nafsi ya kwanza. Katikamistari ya 19-33 anageuka na kutumia nafsi ya tatu katika kuelezea hukuma ya Nebukadneza. Mistari ya 34-37 anabadilika tena na kutumia nafsi ya kwanza katika kuelezea jibu lake kwa Mungu.

Mfalme Nebukadneza aliituma

Kirai hiki kinamrejelea mjumbe wa mfalme kana kwamba ni mfalme mwenyewe. "Mfalme aliwatuma wajumbe wake pamoja"

watu wote, mataifa, na lugha

"watu wote wa kila taifa na lugha"

walioishi katika nchi

Wafalme mara nyingi hutia chumvi kuhusu upana wa ufalme wao ulivyokuwa. Nebukadneza alitawala juu ya sehemu kubwa ya dunia inayojulikana katika kipindi ambacho kitabu hiki kiliandikwa.

amani yenu na iongezeke

Hii ni salaamu ya kawaida.

ishara na maajabu

Maneno haya yana maana sawa na yanarejelea vitu vya kushangaza ambavyo Mungu alikuwa amevifanya.

Ni kwa namna gani Ishara zake ni kubwa, na ni kwa namna gani maajabu yake

Virai hivi viwili vina maana moja na vimetumika katika kutia mkazo juu ya ukubwa wa ishara na maajabu ya Mungu yalivyo.

Ufalme wake ni ufalme unaodumu milele, na utawala wake hudumu kizazi hadi kizaz

Virai hivi vina maana moja na vimerudiwa ili kutia mkazo jinsi utawala wa Mungu ni wa milele.

Daniel 4:4

Maelezo ya jumla

Katika mistari ya 1-18 Nebukadneza anaelezea maono yake kutoka kwa Mungu kwa kutumia nafsi ya kwanza.

nilikuwa ninaishi kwa furaha katika nyumba yangu, na nilikuwa nikifurahia mafanikio

Virai hivi viwili viko sambamba na vinamaanisha kitu kile kile.

nyumba yangu ....ikulu yangu

Virai hivi kimsingi vina maana moja.

ndoto...taswira...maono...

Maneno haya yana maana moja tu kimsingi.

iliniogopesha....ilinitaabisha

Virai hivi viko sambasamba vina maana moja

watu wote wa Babeli walio na hekima

"wote wenye hekima katika Babeli"

Daniel 4:7

Maelezo ya jumla

katika mstari 1-18, Nebukadneza anaelezea maono yake kutoka kwa Mungu kwa kutumia nafsi ya kwanza.

huitwa Belteshaza

Maneno haya yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "ambaye nilimwita Belteshaza."

Belteshaza

Hili ni jina ambalo Wababeli walimpa Danieli.

roho ya miungu watakatifu

Nebukadneza aliamini kwamba nguvu za Danieli zilitokana na miungu ya uongo ambayo Nebukadneza aliiabudu.

hakuna siri iliyo ngumu kwako

tungo hii yaweza kuelezwa kwa kauli ya kukubali. "wewe unafahamu maana ya kila siri"

Daniel 4:10

Maelezo ya jumla

Katika mistari ya 1-18, Nebukadneza anaeleza maono yakekutoka kwa Mungu katika nafsi ya kwanza.

niliyoyaona

mambo ambayo unayoyaona

urefu wake ulikuwa ni mkubwa sana

"ulikuwa ni mrefu sana"

Na sehemu ya juu yake ilifika mbinguni, uliweza kuonekana kutoka miisho ya dunia yote.

Hii ni lugha ya mfano ambayo inatia chumvi juuu ya jinsi mti ulivyokuwa mrefu na jinsi ambavyo mti ulikuwa unajulikana. "Inaonekana kwamba sehemu ya juu ya ti ilifika angani na ya kwamba kila mtu katika dunia aliweza kuuona."

matunda yake yalikuwa ni mengi

"kulikuwa na matunda mengi katika mti"

chakula kwa ajili ya wote

"kilikuwa chakula cha watu wote na wanyama"

Daniel 4:13

Maelezo ya jumla

Katika mistari ya 1-18, Nebukadneza anaeleza maono yake kutoka kwa Mungu katika nafsi ya kwanza.

niliona katika akili zangu

Hii inarejelea kitendo cha kuiona ndoto au maono.

Alipiga kelele na kusema

Inaweza kuwekwa wazi kwamba mjumbe mtakatifu alikuwa akiongea na mtu zaidi ya mmoja

Wanyama na wakimbie kutoka chini yake na ndege wapae mbali kutoka katika matawi yake.

"Wanyama watakimbia chini yake na ndege watapaa kutoka katika matawi yake."

Daniel 4:15

Maelezo ya jumla

Katika mistari ya 1-18, Nebukadneza anaeleza maono yake kutoka kwa Mungu katika nafsi ya kwanza

Maelezo ya jumla

Mjumbe mtakatifu katika maono anaendelea kupiga kelele kwa baadhi ya watu.

kisiki cha mizizi yake

Hii ni sehemy ya mti ambayo huuchwa ardhini baada ya mti kukatwa.

umande

huu ni unyevu nyevu juu ya nchi ambao unapatikana wakati wa asubuhi.

Akili yake na ibadilishwe kutoka... mpaka ipite miaka saba

Kwa kuwa mti unamwakilisha Nebukadneza, kwa hiyo viwakilishi vyote vimetumika katika kifungu hiki kumwongelea yeye.

Daniel 4:17

Maelezo ya jumla

Katika mistari ya 1-18, Nebukadneza anaeleza maono yake kutoka kwa Mungu katika nafsi ya kwanza

Ni uamuzi uliofanya na yeye aliye mtakatifu

Kauli hii yaweza kuelezwa katika muundo tendaji. "Yeye aliye mtakatifu amefanya uamuzi."

mtakatifu

Kirai hiki huenda kinawarejelea Malaika. "Malaika watakatifu"

hao walio hai

"kila mtu aliye hai" au "kila mtu"

huwapa

"huwapa falme"

Belteshaza

Hili ni jina ambalo Wababeli walimpa Danieli.

anayeweza kunitafsiria

"wewe unaweza kuitafsiri ndoto"

roho ya miungu watakatifu

Nebukadneza aliamini kuwa nguvu za Danieli zilitoka kwa miungu ya uongo ambayo yey aliiabudu. Hii haina maana moja na "yey aliye mtakatifu" katika mstari wa 17.

Daniel 4:19

Maelezo ya jumla

katika mistari ya 19-33 inatumia nafsi ya tatu katitka kuelezea hukumu ya Nebukadneza.

Ndipo Danieli aliyeitwa pia Belteshaza

hii nayo yew Ambaye mimi nilimwita Belteshaza

Ufahamu wa Danieli juu ya maono ndiyo yalimwasha.

ndoto hii na iwe kwa ajili ya watu wanaokuchukia, na tafsiri yake na iwe kwa ajili ya adui zako.

ndoto hii na iwe kwa ajili ya watu wanaokuchukia, na tafsiri yake na iwe kwa ajili ya adui zako

Danieli anazungumza matakwa yake kwamba ndoto hii haimhusu mfalme, ingawa alijua kuwa ndoto ilimhusu mfalme.

Daniel 4:20

Maelezo ya jumla

Mistari ya 19-33 inatumia nafsi ya tatu kuelezea hukumu ya Nebukadneza

Maelezo ya jumla

Maneno mengi katika mistari hii inafanana kama katika 4:10

mengi

"mengi sana"

huu mti ni wewe, mfalme,

"mti huu unakuwakilisha wewe mfalme"

Ukuu wako umeongezeka na kufika mbinguni, na mamlaka yako yamefika hata miisho ya dunia.

Virai hivi viwili vina maana sawa

Ukuu wako umeongezeka

Kirai hiki kinatumia neno "kuongezeka" kama njia ya kuuzungumzia ukuu wa mfalme uliokua.

mbinguni... hata miisho ya dunia

Virai hivi viwili vinatia chumvi kwamba kila mtu kila mahali alijua namna ambavyo Nebukadneza alikuwa mkubwa.

Daniel 4:23

Maelezo ya jumla

Mistari ya 19-33 inatumia nafsi ya tatu kuelezea hukumu ya Nebukadneza

Maelezo ya jumla

Mistari hii inafanana sawa sawa kama 4:13 na 4:15

kisiki cha mizizi yake

Hii ni sehemu ya mti ambayo huachwa juu ya ardhi baada ya mti kukatwa.

katikati ya mche mororo katika shamba

"imezungukwa na miche nyororo ya shamba"

umande

"unyevu nyevu ulio katika nchi wakati wa asubuhi"

Daniel 4:24

Maelezo ya jumla

Mistari ya 19-33 inatumia nafsi ya tatu kuelezea hukumu ya Nebukadneza

Maelezo ya jumla

Maneno mengi katika mistari hii inafanana sawa sawa kama 4:15

ambalo limekufikia

"ambalo umelisikia"

Utafukuzwa utoke miongoni mwa watu,

Maneno haya yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Watu watakufukuza utoke miongoni mwao."

Utafanywa uwe unakula majani

Hii yaweza pia kuelezwa kwa muundo tendaji. "utakula majani"

Daniel 4:26

Maelezo ya jumla

Mistari ya 19-33 inatumia nafsi ya tatu kuelezea hukumu ya Nebukadneza

mbingu inatawala

Mahali hapa neno "mbingu" linamrejelea Mungu ambaye anaishi mbinguni. "Mungu wa mbingu ni mtawala wa wote"

ushauri wangu na ukubalike kwako

Maneno haya yaweza kuelezeka kwa muundo tendaji. " tafadhali pokea ushauri wangu"

Geuka uache uovu wako

kukataa uovu kunasemwa kna kwamba ni kugeuka na kuuacha.

walioonewa

Nomina kivumishi hiki kinarejelea watu walioteswa

na itakuwa kwamba mafanikio yako yataongezwa

Muundo tendaji waweza kutumika. "Mungu aweza kuongeza mafanikio yako"

Daniel 4:28

Maelezo ya jumla

Mistari ya 19-33 inatumia nafsi ya tatu kuelezea hukumu ya Nebukadneza

Vitu hivi vyote...katika Babeli

Maelezo katika 4:38 yamepangwa upya ili kwamba maana yake ieleweke kwa urahisi.

miezi wa kumi na miwili

"miezi 12"

Je hii si Babeli kuu....kwa ajili ya utukufu wa enzi yangu?

Nebukadneza anauliza swali hili kwa kutia mkazo katika utukufu wake mwenyewe. Maneno haya yaweza kuelezwa kwa maelezo. "Hii ni Babeli kuu...kwa utukufu wa enzi yangu."

kwa ajili ya utukufu wa enzi yangu

"kuwaonesha watu heshima yangu na ukuu wangu"

Daniel 4:31

Maelezo ya jumla

Mistari ya 19-33 inatumia nafsi ya tatu kuelezea hukumu ya Nebukadneza

Wakati maneno yakali katika midomo ya mfalme

Nahau hii ina maana kwamba wakati mfalme akiwa akiongea

sauti ilisikika kutoka mbinguni

"alisikia sauti kutoka mbinguni"

"Mfalme Nebukadneza.... umeondolewa kutoka kwako

Maneno haya yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Mfalme Nebukadneza, amri imetoka kinyume na wewe kuwa ufalme huu si miliki yako"

Utafukuziwa mbali kutoka miongoni mwa watu

Kauli hii yaweza kuelezeka kwa muundo tendaji. "Watu watakufukuza uende mbali nao"

mtu yeyote amtakaye

"Yeyote amchaguaye"

Daniel 4:33

Maelezo ya jumla

Mistari ya 19-33 inatumia nafsi ya tatu kuelezea hukumu ya Nebukadneza

Agizo hili kinyume na Nebukadneza lilitekelezwa ghafla

Sentensi hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Amri hii iliyo kinyume na Nebukadneza ilitokea ghafla"

Aliondolewa miongoni mwa watu

Sentensi hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Watu walimfukuzia mbali mfalme atoke kwao"

makucha yake yalikuwa kama makucha ya ndege

"Makucha yake ya vidole yalionekana kama makucha ya ndege"

Daniel 4:34

Maelezo ya jumla

Katika mistari ya 34-37 Nebukadneza anaongelea katika nafsi ya kwanza katika kueleza jibu lake kwa Mungu.

katika mwisho wa siku

Hii inarejelea miaka saba katika 4:31

utimamu wa akili nilirudishiwa

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "utimamu wangu ulirudi kwangu"

nilimheshimu na kumtukuza

Maneno yote yanarejelea kitendo kile kile

Kwa kuwa utawala wake ni wa milele, na ufalme wake unadumu katoka katika vizazi vyote hadi vizazi vyote.

Virai vyote viwili vinamaanisha kimsingi kitu kile kile na vimetumika kwa kutia mkazo juu ya jinsi utawala wa Mungu usivyo na mwisho.

Daniel 4:35

Maelezo ya jumla

Katika mistari ya 34-37 Nebukadneza anaongelea katika nafsi ya kwanza katika kueleza jibu lake kwa Mungu.

Wenyeji wote wa duniani huhesabiwa na yeye kuwa bure

Sentensi hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Huwahesabu wakaaji wote wa duniani kuwa si kitu"

Wenyeji wote wa duniani

"watu wote katika dunia"

jeshi la mbinguni

"jeshi la malaika huko mbinguni"

hufanya lolote limpendezalo

"lolote linalotimiza kusudi lake" au kila kitu anachotaka kufanya"

Hakuna hata mmoja awezaye kumzuia

Itakuwa na msaada kuongeza maelezo ya ziada. "Hakuna hata mmoja awezaye kumzuia kufanya kile alichoamua kufanya"

Hakuna hata mmoja awezaye kumwambia, "Mbona umefanya hivi?"

Hii yaweza kuelezeka kwa kutumia nukuru isiyo ya moja kwa moja. "Hakuna awezaye kumwuliza kile anachofanya"

Daniel 4:36

Maelezo ya jumla

Katika mistari ya 34-37 Nebukadneza anaongelea katika nafsi ya kwanza katika kueleza jibu lake kwa Mungu.

utimamu wa akili zangu uliponirudia

Mahali hapa utimamu unaongelewa kana kwamba ulikuwa na uwezo wa kurudi kwa nguvu zake.

utukufu wangu na fahari yangu ilinirudia

Mahali hapa utukufu wake na fahari kwa pamoja unaongelewa kana kwamba ulikuwa na uwezo wa kurudi kwa nguvu zake .

utukufu wangu na fahari yangu

Maneno haya yana maana sawa na yametumika kutilia mkazo juu ya ukubwa wa utukufu wake.

watu wenye heshima walitafuta msaada wangu

"Watu wangu wa heshima waliomba msaada wangu tena"

Nilirudishwa kwenye kiti changu cha enzi, na nilipewa ukuu zaidi

Mahali hapamaneno "kiti cha enzi" yanarejelea mamlaka yake ya kutawala. Pia muundo tendaji waweza kutumika. "Nilirudi kutawala ufalme wangu tena, na nilipata ukubwa zaidi."

ninamsifu, ninamtukuza na kumheshimu

Maneno haya matatu kimsingi yana maana moja na yametumika kutia mkazo juu ya jinsi alivyomsifu Mungu.

wanaotembea katika kiburi chao wenyewe.

Kitenzi "kutembea" kinamrejelea mtu anayetenda kwa kiburi.

Daniel 5

Daniel 5:1

Belshaza

Huyu ni mtoto wa kiume wa Nebukadneza ambaye alikuwa mfalme baada ya baba yake.

elfu moja

"kwa 1,000"

alikunywa divai mbele

"alikkunywa divai akiwa mbele za"

vyombo vilivyotengenezwa kwa dhahabu

Hii yaweza kuandikwa kwa muundo tendaji. "vyombo vya dhahabu au fedha ambavyo waisraeli walikuwa wamevitengeneza"

vyombo

Hivi vilikuwa vikombe na vifaa vingine ambavyo vilikuwa vidogo kwa mtu kuvishikilia na kuvinywea.

Nebukadneza baba yake alikuwa amevichukua

Kirai hiki kinatumia jina Nebukadneza kurejelea jeshi la mfalme. "Jeshi la Nebukadneza baba yake walikuwa wamevichukua"

Daniel 5:3

vyombo ya dhahabu vilivyokuwa vimechukulia katika hekalu,

Muundo tendaji waweza kutumika. "vyombo vya dhahabu ambavyo jeshi la Nebukadneza walikuwa wamevichukua kutoka katika hekalu"

kutoka hekaluni, nyumba ya Mungu

Kirai "nyumba ya Mungu" kinatueleza kitu zaidi juu ya hekalu.

Daniel 5:5

Kwa wakati huo huo

"Mara baada ya kufanya hivyo" au "ghafla"

ukuta uliopigwa lipu

saruji au udongo uliosambazwa katika ukuta au darini ili kuleta ulaini katika sehemu ya juu baada ya kukauka

uso wa mfalme ulibadilika

Hii ilisababishwa na hofu yake

magoti yake yalikuwa yakigongana kwa pamoja

Haya yalikuwa ni matokeo ya hofu yake kubwa.

Daniel 5:7

wale waliojulikana kwa hekima katika Babeli

Hii inarejelea nyuma kwa wale watu wanaodai kusema na wafu, watu wenye hekima na wanajimu

Yeyote atakayeyaeleza maandishi haya na maana yake atavikwa nguo za zambarau na atavikwa na mkufu wa dhahabu shingoni mwake

Kauli hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Nitampa nguo za zambarau na shingo ya dhahabu kwa yeyote atakayeyaeleza maandishi yake na maana yake."

atavikwa nguo za zambarau

Nguo za dhahabu zilikuwa adimu na zilitunzwa maalumu kwa ajili maafisa wa kifalme.

mtawala wa tatu wa juu

"mtawala namba tatu"

Daniel 5:8

Belshaza

Hili lilikuwa ni jina la mtoto wa kiume wa Nebukadneza ambaye alikuwa mfalme baada yake.

mwonekano wa uso wake ulibadilika

Uso wa mfalme uliendelea kuonekana dhaifa na hafifu kuliko hata ulivyokuwa katika 5:5

walishangazwa

"kuchanganyikiwa"

Daniel 5:10

Malkia

Matoleo ya kisasa huelewa hili kuwa ni rejea kwa mama malkia, ambaye ni mama wa mfalme. Mama malkia alipewa heshima kubwa katika Babeli ya zamani.

Mfalme na aishi milele

Hii ilikuwa ni njia ya kawaida ya kumsalimia mfalme.

Usiuruhusu mwonekano wa uso wako ubadilike.

"Hakuna haja ya uso kubadilika na kuwa dhaifu"

Daniel 5:11

roho ya miungu watakatifu

Malkia aliamini kwamba nguvu za Danieli zilitoka kwa miungu ya uongo ambayo Nebukadneza aliiabudu.

Katika siku za baba yako

"Wakati ambao baba yako alikuwa akitawala"

mwanga na weledi na hekima ya miungu ilipatikana ndani yake

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "alikuwa na mwanga na ufahamu na hekima kama hekima ya miungu"

Mfalme Nebukadneza, baba yako mfalme

"Baba yako Mfalme Nebukadneza"

hizi ni sifa zilizopatikana kwa mtu huyu Danieli, ambaye mfalme alimwita Belteshaza.

Muundo tendaji waweza pia kutumika."huyu Danieli ambaye mfalme alimwita Belteshaza, alikuwa na sifa hizi zote."

kile kilichoandikwa

"kile kilichokuwa kimeandikwa ukatani"

Daniel 5:13

Ndipo Danieli alipoletwa mbele ya mfalme

Hii yaweza kuelezwa kwa kutumia muundo tendaji. "Kisha walimleta Danieli mbele ya mfalme" au "wanajeshi walimleta Danieli mbele ya mfalme"

ambao baba yangu mfalme aliwaleta kutoka Yuda

Katika kirai hiki, neno "baba" limetumika kumaanisha wanajeshi wote.

roho ya miungu

Belshaza aliamini kuwa nguvu za Danieli zilitoka kwa miungu ya uongo ambayo Belshaza aliiabudu.

mwanga na ufahamu na hekima bora inapatikana ndani yako

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "una mwanga na ufahamu na hekima bora"

Daniel 5:15

Na sasa watu wanaojulikana ....wamekwisha kuletwa mbele yangu

Muundo tendaji waweza kutumika pia."sasa watu waliojulikana ....wamekuja mbele yangu"

kunijulisha

"kuniambia"

utavikwa nguo za zambarau na kuwa na kuvalishwa mkufu wa dhahabu shingoni mwako

Maneno haya yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji."Nitakupatia nguo za zambarau na mkufu wa dhahabu shingoni"

utavikwa nguo za zambarau

Nguo za zambarau zilikuwa ni adimu na zilitunzwa kwa ajili ya maafisa wa kifalme.

mtawala wa tatu

"mtawala wa namba ya tatu"

Daniel 5:17

Zawadi yako na iwe kwa ajili yako

"Sihitaji zawadi zako"

watu wote, mataifa, na lugha

Kirai hiki kina neno "wote" ili kuwakilisha namba kubwa.

walimtetemekea na kumwogopa

Maneno haya kimsingi yanamaanisha kitu kile kile na yametumika kwa ajili ya kutia mkazo juu ya ukubwa wa hofu.

Aliwauwa wale aliotaka wafe

Kirai hiki cha maneno hakina maana ya kwamba mfalme Nebukadneza hakuwauwa watu yeye mwenyewe, bali wale aliowaagiza.

Aliwainua wale aliowataka

"Aliwainua wale aliowataka kuwainua"

aliwashusha wale aliowataka.

"aliwashusha wale aliotaka kuwashusha"

Daniel 5:20

moyo ulipokuwa na kiburi

Mahali hapa neno "moyo" linamrejelea mfalme mwenyewe.

roho yake ilifanywa kuwa mgumu

Mahali neno "roho" linamaanisha mfalme mwenyewe. Kiburi chake kinasemwa kana kwamba kilikuwa kimefanywa kuwa kigumu.

kwa kiburi

"kwa kiburi na zaidi ya kujiamini

alishushwa kutoka kiti chake cha enzi cha kifalme

Mahali "kiti cha enzi" kina maana ya mamlaka yake ya kutawala. Hii pia yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Watu waliutwaa ufalme wake."

Aliondolewa katika ubinadamu

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. Watu walimfukuza atoke kati yao"

alikuwa na akili za mnyama,

Mahali hapa neno "akili" lina maana ya mawazo. "Alifikiri kama vile mnyama anavyofikiri"

umande

Ni unyevu nyevu ulio juu ya nchi ambao hupatikana nyakati za asubuhi.

yeyote amtakaye

"yeyote amchaguaye"

Daniel 5:22

Belshaza

Hili lilikuwa ni jina la mtoto wa kiume wa Nebukadneza ambaye alikuwa mfalme baada yake

haujaunyenyekeza moyo wako

Mahali hapa neno 'moyo' linamwakilisha Nebukadneza mwenyewe.

umwenyewe kinyume cha Bwana

Kitendo cha kuasi kinyume na Mungu kinasemwa kana kwamba ni kujiinua mtu mwenyewe.

kutoka katika nyumba yake

Kirai "nyumba yake" kinaeza kuelezwa kwa uwazi sna "kutoka kwa hekalu la mfalme."

njia zako zote"

"kila kitu uanchokifanya"

Mungu ambaye anaishikilia pumzi yako katika mkono wake

Mahali hapa neno 'pumzi" lina maana ya fedja ma memp "mkono" lina maana ya mamlaka au utawala.

maandishi haya yaliandikwa

Muundo tendaji waweza kutumika. "iliandika ajumbe huu"

Daniel 5:25

Haya ndiyo maandishi ambayo yaliandikwa

Kwa kutumia muundo tendaji twaweza kusema. " huu ni ujumbe ambao uliandikwa na mkono"

'Mene, Mene, Tekeli na Peresin.

Haya ni maneno ya Kiramaiki ambayo yalikuwa yameandikwa ukutani.

'Mene,' 'Mungu ameuhesabu

"mene' ina maana ya kuwa Mungu amehesabu"

Tekeli' 'umepimwa katika mizani

"Tekeli' ina maana ya wewe umepimwa"

Peresi' 'ufalme wako

"Peresi" ina maana ya ufalme wako

'umepimwa katika mizani na umeonekana umepungua

kuhukumu na kuamua juu ya uthamani kwa mfalme katika kutawala unasemwa kana kwamba ni kumpima. Hii ina maana ya kwamba mfalme hafai kuongoza/kutawala.

'ufalme wako umegawanyika na wamepewa Wamedi na Waajemi.'"

Kwa kutumia muundo tendaji twaweza kusema. "Mungu ameugawa ufalme wako na amewapa Wamedi na Waajemi.

Daniel 5:29

Mkufu wa dhahabu walimvisha shingoni

Hii yaweza kuelelzwa kwa muundo tendaji. " Waliuweka mkufu wa dhahabu shingoni mwake"

mtawala mwenye mamlaka ya nafasi ya tatu

"mtawala wa namba ya tatu"

aliuchukua ufalme

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "alikuwa mtawala wa ufalme"

alipokuwa na miaka ipatayo sitini na miwili.

"wakati alipokuwa takribani miaka 62"

Daniel 6

Daniel 6:1

Sentensi kiunganishi

Matukio katika sura hii yalitukia baada ya Waajemi kuwaangusha Wababeli na Dariuo Mmedi alianza kutawala juu ya Babeli.

Ilimpendeza Dario

"Mfalme Dario aliamua"

magavana wa majimbo 120

"Magavana wa majimbo wapatao mia na ishirini"

juu yao

Neno 'wao' linawarejelea magavana 120

ili kwamba mfalme asipate hasara.

"ili kwamba chochote kisiibiwe kutoka kwa mfalme"

alipambanuliwa juu

"alifaulu juu ya " au " alikuwa na uwezo kuliko"

likuwa na roho isiyo ya kawaida

Mahali hapa "roho" inamrejelea Danieli. Inamaanisha kuwa kile alichokuwa nacho kilikuwa si cha kawaida kwa watu. "alikuwa ni mtu wa kipekee"

isiyo kawaida

"ya kuvutia" au "bora"

kumweka juu ya

"kumpa mamlaka juu ya " au " kumweka kuwa masimamizi wa "

Daniel 6:4

Basi watawala wakuu wengine na magavana wa majimbo .... kwa ufalme

Watawala wengine walimwonea Danieli wivu. Hii yaweza kuwekwa dhahiri. "kisha watawala wengine na magavana wa majimbo walikuwa na wivu. Hivyo, wakatafuta makosa katika kazi za Danieli alizozifanya kwa ajili ya ufalme. "

Hakuna kosa au uzembe uliopatikana ndani yake

Maneno haya yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Hawakuweza kupata makosa au uzembe katika kazi yake."

kumshitaki huyu Danieli

"kumlalamikia Danieli"

Daniel 6:6

walileta mpango mbele ya mfalme

"waliwasilisha mpango kwa mfalme"

Mfalme Dario, uishi milele!

Hii ilikuwa ni njia ya kawaida ya kumsalimia mfalme.

siku thelathini

"kwa siku 30"

mtu yeyote anayefanya dua

"yeyote atakayetoa ombi"

mtu huyo lazima atupwe katika tundu la simba

Maneno haya yaweza kuelezeka kwa muundo tendaji. "wanajeshi wako lazima wamtupe mtu huyo katika tundu la simba"

tundu la simba

Hii inarejelea chumba au shimo mahali ambapo simba walikuwa wametunzwa

Daniel 6:8

Sentensi kiunganishi

Katika mstari wa 8, watawala wanaendelea kuongea na mfalme

kama ilivyoelekezwa katika sheria

"kutokana na sheria"

haiweze ikabatilishwa

"haiwezi kusitishwa"

kuifanya amri kuwa sheria

"kulifanya agizo kuwa sheria"

Daniel 6:10

Danieli alipojua kuwa nyaraka imekwisha kusainiwa kuwa sheria

Ni muhimu katika habari hii kueleza wazi kwamba Daniel alijua juu ya sheria mpaya kabla hajamwomba Mungu.

madirisha yake katika chumba cha juu yalikuwa wazi kuelekea Yerusalemu

Haya ni maelezo ya muhimu ambayo yanaelezea jinsi maadui wa Danieli walijua kuwa Danieli alikuwa akiomba kwa Mungu wake.

kushukuru mbele ya Mungu wake,

"alitoa shukrani kwa Mungu wake"

hila

mpango wenye kusudi ovu

Daniel 6:12

Je .haukuweka amri ....simba?

Walimwuliza swali hili ili kumfanya mfalme ahakikishe kuwa alikuwa ametoa amri.

mtu yeyote akayefanya maombi

"ambaye afanyaye maombi"

tundu la simba

Hii inarejelea chumba au shimo mahali simba walikuwa wanatunzwa.

kama ilivyoelekezwa katika sheria

"kutokana na sheria"

Daniel 6:13

Mtu yule Danieli

Hii si njia ya heshima ya kumzungumzia Danieli. Walitumia maelezo haya kimakusudi ili kutompa Danieli heshima aliyostahili kama mtawala mkuu.

ambaye ni mmoja wa watu wa mateka kutoka Yuda,

"ambaye ni mhamiaji kutoka Yuda"

hakutii wewe

Hii ni nahau inayoonesha kuwa anakatalia Mfalme "Hakutii wewe"

, alitumia akili

Mahali hapa neno "akili"linarejelea fikra zake.

Alisumbuka sana

Hii inarejelea masumbuko ya kiakili badala ya masumbuko ya kimwili.

Daniel 6:15

hakuna amri....yaweza kubadilishwa

maelezo ya ziada yaweza kuongezwa hapa ili kusaidia ufahamu. "hakuna amri... yaweza kubadilishwa. Lazima wamtupe Danieli katika shimo la simba"

Daniel 6:16

walimleta ndani Danieli

"wanajeshi wake walienda na kumleta Danieli"

tundu la simba

Hii inarejelea chumba au shimo mahali simba walikuwa wanatunzwa.

Mungu wako..... na akuokoe

Mfalme anaelezea matakwa yake kwa ya Mungu kumwokoa Danieli.

akuokoe

"kukuokoa kutoka katika simba"

Daniel 6:17

tundu

Hii inarejelea chumba au shimo mahali simba walikuwa wanatunzwa.

mfalme alilitia muhuri wa pete yake mwenyewe na pamoja na muhuri wa wakuu wake.... kuhusiana na Danieli

Kazi ya pete yea muhuri yaweza kuelezewa kwa uwazi. Mfalme pamoja na wakuu wake walikandamiza pete katika chapa iliyotengenezwa kwa nta.

na usiku ule alikuwa na mfungo

Hili ni tendo linaloashiria kwamba mfalme alikuwa na wasiwasi kuhusu Danieli.

chochote kisiweze kubadilishwa kuhusiana na Danieli

"hakuna awezaye kumsaidia Danieli"

Hakuna starehe yoyote iliyoletwa mbele yake

maneno haya yaweza kuelezwa kwa kutumia muundo tendaji. " Hapakuwa na mtu yeyote wa kumburudisha"

nao usingizi ulimkimbia

Usingizi unaongelewa kana kwamba unaweza kukimbia kutoka kwa mfalme. "hakulala kabisa usiku wote ule"

Daniel 6:19

tundu la simba

Hii inarejelea chumba au shimo mahali simba walikuwa wanatunzwa.

Daniel 6:21

Kwa kuwa sikuwa na hatia yoyote

Muundo tendaji waweza kutumika. " Anajua kuwa sijafanya chochote kibaya"

sijakufanyia jambo lolote la kukudhuru

"Sijakudhuru wewe kabisa"

Daniel 6:23

tundu la simba

Hii inarejelea chumba au shimo mahali simba walikuwa wanatunzwa

Hakuna dhara lolote lililoonekana kwake

Maneno haya yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Hawakuona jeraha lolote kwa Danieli"

Daniel 6:24

tundu la simba

Hii inarejelea chumba au shimo mahali simba walikuwa wanatunzwa

Kabla hawajafika sakafuni

"kabla hawajafika chini katika tundu la simba"

kuvunjavunja mifupa yao vipande vipande

"kuvunja mifupa yao"

watu wote, mataifa na lugha

"watu wa mataifa yote na lugha"

katika dunia yote:

Mfalme Dario aliandika ujumbe huu kwa ufalme wake wote ulikuwa mkubwa. Hapa anatumia maneno "dunia yote" kutilia mkazo juu ya ukubwa wa ufalme wake ulivyokuwa, ingawa haukuwa kwa watu wote wa duniani"

Amani na iongezeke kwenu

Huu ni muundo wa salaamu iliyotumika kwa kumtakia mtu mema katika sehemu zote za maisha.

Daniel 6:26

Maelezo kiunganishi

Hii inaendelea kueleza ujumbe ambao Dario aliutuma kwa kila mtu katika ufalme wake.

watetemeka na kumcha

Maneno haya yana maana sawa na yanaweza kuunganishwa. "kutetemeka kwa hofu"

Mungu wa Danieli

"Mungu ambaye Danieli alimwabudu"

kwa kuwa ni Mungu aliye hai na huishi milele

Virai hivi viwili "Mungu aliye hai" na "aishiye milele" vinaelezea dhana moja, kwamba Mungu huishi milele.

ufalme wake ha....; utawala wake uta..

Virai hivi vyote viko sambasamba, na vinatia nguvu juuu ya jinsi ufalme wa Mungu hautakuwa na mwisho."

ufalme wake hauwezi kuharibiwa

Maneno haya yaweza kuelezwa katika muundo tendaji. " hakuna yeyote aweza kuuangusha ufalme wake" au "ufalme wake utadumu milele"

utawala wake utakuwepo hadi mwisho.

"atatawala milele"

amemhifadhi Danieli salama dhidi ya uwezo wa simba.

"hajawaruhusu simba wenye nguvu kumdhuru Danieli"

Daniel 6:28

atika utawala wa Dario na katika utawala wa Koreshi Mwajemi

Koreshi Mwajemi alikuwa mfalme aliyetawala baada ya Dario.

Daniel 7

Daniel 7:1

Maelezo ya jumla

Sura ya 7 na ya 8 haziko katika mpango wa mtiririko wa kawaida. Zilitokea wakati Belshaza alipokuwa akali ni mfalme, kabla ya utawala wa Dario na Koreshi walioongelewa katika sura ya 6.

Maelezo ya jumla

Katika maono ya Danieli, aliona wanyama waliokuwa ni ishara ya mambo mengine. Baadaye katika maono mtu fulani alifafanua maana ya ishara hizo.

Belshaza

Hili ni jina la mtoto wa kiume wa Nebukadneza, ambaye alikuwa mfalme baada yake.

ndoto na maono

Maneno haya "ndoto na maono" yote yanarejelea ndoto ile ile iliyoelezewa katika sura hii.

pepo nne za mbinguni

"pepo kutoka kila sehemu" au "pepo zenye nguvu kutoka sehemu zote nne za mwalekeo"

zinaitikisa

"piga piga" au "kusababisha mawimbi makubwa"

Daniel 7:4

Mnyama wa kwanza alikuwa kama simba

Huyu ni mnyama wa ishar, na si mnyama halisi anayeishi.

mabawa yake yalikuwa yamepasuka na alikuwa ameinuliwa katika ardhi na alikuwa amesimama kwa miguu miwili kama mtu

Maneno haya yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "mtu fulani alipasua mabawa yake na kumwinua kutoka chini na kumifanya asimame kwa miguu miwili kama binadamu."

Na alipewa akili za kibinadamu

Mahali hapa neno "akili" limetumika kumaanisha "fikra.' Muundo tendaji waweza kutumika. "Mtu fulani alimpa uwezo wa kufikiri kama mtu"

kulikuwa na mnyama wa pili, alikuwa kama dubu

Huyu hakuwa dubu halisi, bali ni mnyama wa ishara ambaye alifanana na dubu.

mbavu

Mifupa mikubwa ya kifuani iliyopinda ambayo imeungana na uti wa mgongo.

aliambiwa

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Mtu fulani alimwambia"

Daniel 7:6

mnyama mwingine ambaye alionekana kama chui

Huyu hakuwa chui halisi, bali mnyama wa ishara ambaye alikuwa akifanana na chui.

mabawa manne ....vichwa vinne

Mabawa manne na vichwa vinne ni mifano/ishara, lakini maana zake haziko wazi.

alikuwa na vichwa vinne.

"mnyama alikuwa na vichwa vinne"

Alipewa mamlaka ya kutawala

Kauli hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Mtu fulani alimpa mamlaka ya kutawala"

mnyama wa nne...alikuwa na pembe kumi

Huyu pia si mnyama halisi. Ni mnyama wa mfano.

kusaga saga katika miguuni

"kutembea juu yake na kuvunja vunja''

Daniel 7:8

Maelezo ya jumla

Danieli anaendelea kuyaelezea maono yake ya mnyama wa nne ambayo aliyoyaona katika 7:6

pembe

Watafsiri waweza kuandika tanbihi chini ya ukurasa. "Pembe" ni alama au ishara ya ngur

Mizizi ya pembe tatu kati ya pembe za mwanzo iling'olewa

Tungo hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Pembe ndogo ilichomoza kati ya pembe tatu za mwanzo."

mdomo ambao ulikuwa ukijivuna kwa mambo makubwa.

Mahali hapa kuna pembe ilikuwa inajivuna kwa kutumia mdomo wake. "pembe ilikuwa na mdomo na ulijivuna kuhusu kufanya mambo makubwa"

Daniel 7:9

Maelezo ya jumla

Vifungu vingi vya mistari 9-14 ni lugha ya picha ikiwa na mistari sambamba iliyo na maana sawa.

viti vya enzi vilikuwa vimewekwa

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. " mtu fulani aliviweka viti vya enzi katika sehemu zake"

Mtu wa Siku za Kale

Hili jina la Mungu ambalo lina maana kwamba yeye ni wa milele.

alikaa sehemu yake...mavazi yake... nywele zake

"Kifungu hiki kinamwelezea Mungu akiwa amekaa, akiwa na mavazi na nywele kama mtu. Hii haina maana kwamba Mungu yuko hivyo, bali ni vile ambavyo Danieli alivyomwona Danieli katika maono.

alikaa sehemu yake

Hii ni lugha ya picha ikiwa na maana ya kwamba Mungu alikaa katika kiti chake cha enzi.

Mavazi yake yalikuwa meupe kama theruji

Mavazi yake yanalinganishwa na theruji kuonesha kwamba zilikuwa ni nyeupe sana. "nguo zake zilikuwa nyeupe sana"

ywele zake katika kichwa chake zilikuwa safi kama sufu

nywele za Mungu zilionekana kama sufu. maana zinazokkubalika ni 1) zilikuwa ni nyeupe sana 2) zilikuwa ni nzito na zilizopinda pinda.

sufu safi

"sufu nzuri" au "sufu zilizooh

Kiti chake cha enzi kilikuwa na miali ya moto, na magurudumu yake yalikuwa yanawaka moto

Hii inafafanua juu ya kiti cha enzi cha Mungu na magurudumu yake kana kwamba yalikuwa yametenenezwa kwa moto. Maneo''miali ya moto' na 'kuwaka moto" kimsingi yanamaanisha kitu kile kile na inaweza kufasiriwa kwa namna ile ile.

magurudumu yake

Haiko wazi sana kwanini kiti cha enzi cha Mungu kinaelezwa kuwa na magurudumu. Viti vya enzi kikawaida huwa havina maguruduma, lakini kifungu kwa uwazi kinaelezea kwamba kiti hiki cha enzi kilikuwa na magurudumu.

Daniel 7:10

Maelezo ya jumla

Danieli anaendelea kuelezea maono yake juu ya jibu kutoka mbingu kwa mnyama wa nne ambaye alimwona katika 7:6

Maelezo ya jumla

Vifungu vingi vya mistari ya 9-14 ni lugha ya picha yenye mistari sambamba iliyo na maana sawa.

Mto wa moto ulitiririka kutoka mbele yake

Kitendo cha moto kutoka kwa haraka mbele za Bwana kunasemwa kana kwamba ni maji yanatiririka.

mbele yake

Neno "yake" inamrejelea Mungu, Siku za Kale kutoka 7:9

mamilioni

Hii huenda inarejelea kundi kubwa kulilka hesabu ndogo. "Maelfu elfu" au "hesabu kubwa ya watu"

mia moja milioni

Hii huenda inarejelea kundi kubwa kulilka hesabu ndogo. "makumi elfu mara makumi elfu" au "watu wasio hesabika"

mahakama iliitishwa

Hiii ina maana kwamba Mungu, hakimu, alikuwa tayari kuchunguza ushahidi na kufanya hukumu yake.

vitabu vilifunguliwa

Hivi ni vitabu ambavyo vimejumuisha ushahidi utakaotumika katika mahakama. "vitabu vya ushahidi vilifunguliwa"

Daniel 7:11

Maelezo ya jumla

Danieli anaendelea kuelezea maono yake ya mahakama ya mbinguni katika kujibu mnyama wa nne aliyemwona katika 7:6

mnyama anauliwa...kwa ajili ya kuchomwa moto

Kauli hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "walimwua mnyama wa nne, wakaharibu mwili wake na wakampa mtu fulani ili auchome."

mnyama

Hii inamrejelea mnyama wa nne ambaye alikuwa na pembe kumi na pembe ile iliyojivuna.

Na kwa wale wanyama wanne waliosalia,

Inaweza kuwa wazi kusema, "wanyama wengine watatu"

mamlaka yao yalitwaliwa mbali,

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "hakimu aliyachukua mamlaka yao ya kutawala" au "mamlaka yao ya kutawala yalikoma'

maisha yao yaliendelezea kwa kipindi fulani cha muda

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. " waliendelea kuishi kwa kipindi fulani cha muda" au "hakimu aliwaacha waishi kidogo"

Daniel 7:13

Maelezo ya jumla

Vifungu vingi vya mistari ya 9-14 ni lugha ya picha yenye mistari sambamba iliyo na maana sawa.

nilimwona mtu mmoja anakuja ... kama mwana wa mtu

Mtu ambaye Danieli alimwona hakuwa ni mtu wa kawaida, lakini alikuwa na mwonekano kama wa kibidamu. "Niliona usiku ule mtu fulani ambaye anafanana na na mwana wa mtu, yaani alikuwa na umbo la kibinadamu"

katika mawingu ya mbinguni

"pamoja na mawingu ya angani"

kwa Mzee wa Siku

Hii inamrejelea Mungu ambaye ni wa milele.

aliletwa mbele zake

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. 'walimleta huyu mwana wa mtu kwa Mzee wa Siku" au "alisimama mbele yake"

Naye alipewa mamlaka ya kiutawala na utukufu na mamlaka ya kifalme

Maelezo haya yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. " Yeye aliyeonekana kama mwana wa mtu alipokea mamlaka ya kutawala, utukufu, na nguvu za kifalme."

nguvu za kifalme

Hii inarejelea "mamlaka"

hayatapita,..... hautaangamizwa

Virai hivi viwili vina maana ile ile

ule ambao hautaangamizwa

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. " kwamba hakuna hata mmoja atakayeangamiza"

Daniel 7:15

roho yangu ilihuzunishwa ndani yangu, na maono niliyoyaona katika akili zangu yalinisumbua.

Virai hivi viwili vinaelezea jinsi Danieli alivyokuwa akijisikia. Kirai cha pili kinatoa maelezo ya ziada juu ya kirai cha kwanza, kikieleza juu ya roho inayosumbuka.

roho yangu ilihuzunishwa ndani yangu

Mahali hapa maneno "roho yangu" inamrejelea Danieli mwenyewe. "Nilikuwa na huzuni ndani yangu"

mmoja wa hawa walikuwa wamesimama hapo

Huyu ni moja wa viumbe vya mbinguni aliyekuwa amesimama mbele ya kiti cha enzi cha Mungu. Maana zinazokubalika 1) hawa ni malaika, roho zinazomtumikia Mungu 2) hawa ni watu walikwisha kufa na sasa wako mbinguni.

anioneshe

"kuniambia mimi"

mambo haya

"mambo niliyokuwa nimeyaona"

Daniel 7:17

Hawa wanyama nne wakubwa

"Hawa ni wanyama wakubwa"

ni wafalme wanne

"inawakilisha wafalme wanne"

wafalme wanne ambao watatoa katika nchi

Hapa maneno "kutoka katika nchi" ina maana ya kuwa ni watu wa kawaida.

wataumiliki

"watatawala juu yake"

milele na milele

Haya mawazo ya kujirudia yanatia mkazo kwamba ufalme huu hautakuwa na mwisho.

Daniel 7:19

alikuwa wa kutisha

"wa kuogofya sana"

alisaga saga kwa miguu yake

"alitembea juu yake na kukanyaga"

pembe kumi katika kichwa chake

"pembe kumi juu ya kichwa cha mnyama wa nne"

iliyochomoza, na ambayo mbele yake pembe zingine tatu zilianguka chini

"ilikua na pembe takribani tatu zilianguka chini mbele yake" au "ilichomoza na kuhusu pembe tatu ambazo zilianguka chini kwa sababu yake."

ambayo mbele yake pembe zingine tatu zilianguka chini

Hapa neno "kuanguka chini" ni tafsida ambayo ina maana kwamba ziliteketezwa"

mdomo uliokuwa unajisifu

"mdomo wake wenye kujisifu" au "mdomo wa pembe mpya ambao unajisifu"

ambayo ilionekana kuwa ni kubwa kuliko zingine

pembe yenye macho na mdomo ilionekana kuwa kubwa kuliko pembe zingine

Daniel 7:21

pembe hii

"pembe hii ya nne" Hii inarejelea pembe ambayo imeelezewa katika 7:19

mpaka pale Mzee wa Siku alipokuja, na haki alipewa

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji "mpaka Mzee wa Siku alipokuja na kuleta haki"

Mzee wa Siku

Hili ni jina la Mungu ambalo linatia mkazo kwamba Yeye ni wa milele.

watu watakatifu waliupokea ufalme

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. " Mungu aliwapa watu wake watakatifu ufalme wake"

Daniel 7:23

Maelezo ya jumla

Vifungu vingi vya mistari ya 23-27 ni lugha ya picha.

Hiki ndicho mtu yule alichokisema

Huyu niNa kuhusu pembe kumi mtu ambaye Danieli alimkaribia katika 7:15

mtu yule alichokisema

mtu yule alijibu

Kwa habari ya mnyama wanne...Na kuhusu pembe kumi

"kuhusu mnyama wa nne...kuhusu pembe kumi"

Utaimeza ..... vipande vipande

Hii haina manna kwamba ufalme wa nne utaiharibu sayari, bali ni kwamba utashambulia, kushinda na kuharibu falme zingine zote za duniani.

kutoka katika ufalme huu, wafalme kumi watainuka

Watatawala mmoja baada ya mwingine. Hii yaweza kuwekwa wazi. "wafalme kumi watautwala ufalme wa nne, mmoja baada ya mwingine"

mwingine atainuka baada yao

Mfalme huyu si mmoja wa wale kumi. Ni vizuri kumrejelea kama mfalme wa kumi na moja.

Atakuwa wa tofauti na wale waliomtangulia,

"atakuwa tofauti na waflme wengine kumi"

atawashinda wale wafalme watatu

Atawashinda wafalme halisi watatu. inaeza kusaidia kueleza kuwa wale wafalme watatu wanawakilishwa ba pembe tatu zilizong'olewa.

Daniel 7:25

Maelezo ya jumla

Mtu ambaye Danieli alimwona katika maono anaendele kuongea na Danieli.

Maelezo ya jumla

vifungu vingi vya mistari ya 23-27 vinatumia lugha ya picha.

Atazungumza maneno kinyume cha Yeye Aliye Juu sana

Hii ina maana kwamba mfalme mpya ajaye atamkataa wazi wazi na kusema maneno mabaya juu ya Yeye aliye juu sana.

Atajaribu.....katika mikono yake.

Kiwakilishi "a" na kimilikishi "yake" vinamrejelea mfalme mpaya, siyo Yeye aliye juu sana.

watu watakatifu

Watu wakatifu wa Mungu

kuzibadili sikukuu na sheria.

Maneno yote rana rejelea sheria za Musa. Sikukuu zilikuwa nia muhimu katika masuala ya kidini katika Israeli katika Agano lake.

Mambo haya atapewa mikononi mwake

hapa maneno "mkono wake" inarejelea utawala. Hii yaeza kuelezwa kwa muundo tendaji " Mfalme mpya atatawala sikukuu zote za dini na sheria.

mwaka mmoja, miaka miwili na nusu mwaka.

Hii ina maana ya "miaka mitatu na nusu" Hii si njia ya kawaida ambayo Waisraeli walitumia katika kuhesabu.

mahakama kitaitishwa

Hii ina maana kwamba hakiku atakuwa tayari kuchunguza ushahidi na kufanya hukumu yake.

watazichukua nguvu zake za kifalme

Wanachama katika mahakama watazitwaa nguvu zake za kifalme kutoka mfalme mpya.

nguvu za kifalme

Hii inarejelea "mamlaka"

aweza kuharibiwa na kuteketezwa

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "na kuharibu na kuangamiza mwishoni"

Daniel 7:27

Maelezo ya jumla

Danieli anaendelea kuongea na mtu yule aliyemwona katka maono.

maelezo ya jumla

Vifungu vingi vya mistari ya 23-17 vinatumia lugha ya picha.

Ufalme na utawala....watapewa watu walio wa wat

Hii yaweza kuelezwa kwa muuundo tendaji. "Mungu atawapa watu...ufalme na utawala...

Ufalme na utawala

Maneno haya maweili yana maana ile ile na yanatia mkazo juu ya miundo yote ya mamlaka rasmi

ukubwa wa falme

Nomino dhahania "ukubwa" yaweza kutafsiriwa kwa kivumishi "kubwa"

chini ya mbingu yote

Nahau "chini ya mbingu yote" inarejelea falme juu ya nchi.

ufalme wake

"ufalme wa Mungu aliye juu"

ufalme wa milele

"ufalme ambao utadumi milele" au " ufalme ambao hautakoma"

Na huu ndio mwisho wa mambo

Hii ina maana kwamba Danieli amemaliza kuelezea maono yake.

mwonekano wa uso wangu ulibadilika

"uso wangu ulikuwa dhaifu/hafifu"

Daniel 8

Daniel 8:1

Maelezo ya jumla

Sura ya 7 na ya 8 haziko katika mtiririko maalumu. Zilitokea wakati Belshaza alipokuwa angali ni mfalme, kabla ya utawala wa Dario na Koreshi ambazo zimeongelewa katika sura ya 6.

Maelezo ya jumla

Katika maono ya Danieli, aliona wanyama waliokuwa ni ishara ya mambo mengine. Baadaye katika maono mtu fulani alimwelezea maana ya ishara hizo.

Katika mwaka wa tatu

"Ndani ya mwaka wa tatu"

niliona maono (baada ya maono ya awali yaliyonipata)

Haya ni maelezo ya nyuma ili kumkumbusha msomaji kwamba haya yalikuwa ni maono ya pili kwa Danieli.

Belshaza

Huyu ni mtoto wa kiume wa Nebukadneza ambaye alikuwa mfalme baada ya baba yake.

ngome

kulindwa na kuhifadhiwa

Shusha....Elamu...Mfereji wa Ulai

Haya ni majina ya sehemu/mahali

Mfereji

Mfereji ni njia nyembamba ya maji iliyotengenezwa na mwanadamu.

Daniel 8:3

kondoo dume lenye mapembe mawili

kondoo dume lenye mapembe mawili ni kawaida kwa beberu kuwa na pembe mbili. ingawa, Mapembe haya yana maana yanayoiashiria.

lakini pembe ndefu .....ilirefuka na kuizidi nyingine.

"lakini pembe ndefu ilikua pole pole kuliko ile fupi, na pembe fupi ilikua na kuwa ndefu kuliko ile."

Niliona kondoo mme akiishambulia

"Nilimwona kondoo mme akiharakisha" au "nilimwona beberu akikimbia kwa haraka sana"

kumwokoa yeyote katika mkono wake

"Beberu huwa hazina mikono. Mahali hapa "mkono" unarejelea 'nguvu za kondoo"

Daniel 8:5

kuvuka katika uso wa dunia yote

Mahali hapa neno "uso" linarejelea sehemu ya juu ya nchi. Kirai "dunia yote" kinatia chumvi chenye maana kwamba alikuja kutoka mbali sana.

Mbuzi huyo alikuwa na pembe kubwa katikati ya macho yake

Mbuzi huwa na pembe mbili katika pande mbili za vichwa vyao. Sura hii lazima ielezeke kama "Mbuzi alikuwa na pembe moja kubwa katikati ya kichwa chake"

nilikuwa nimemwona kondoo dume amesimama katika ukingo wa mfereji

Kirai hiki kimechomekwa ili kuleta maelezo ya nyuma ili kuelezea mahali ambapo beberu alikuwa.

kwa hasira kali

"na alikuwa na hasira kali"

Daniel 8:7

akamkanyaga

Kukanyaga kitu fulani kwa kutembea juu yake.

kutoka katika nguvu zake

"kondoo kutoka kwa mbuzi kwasababu ya nguvu zake"

mbuzi alikua akawa mkubwa

"mbuzi alikuwa mkubwa na mwenye nguvu"

pembe kubwa ilivunjwa,

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Kitu fulani kiliivunja pembe kubwa"

kuelekea pepo nne za mbingu.

Mahali hapa "pepo nne za mbinguni" ni nahau inayorejelea pembe kuu nne (kaskazini, mashariki, magharibi na kusini) kutoka huko pepo huvuma.

Daniel 8:9

ilikuwa pembe kubwa

"lakini ilikuwa kubwa sana"

upande wa kusini, na mashariki, na katika nchi ya uzuri

Hii huenda ina maana ya kwamba pembe imeelekea sehemu hizo. "na imeelekea upande wa kusini na kisha upande wa mashariki na kisha nchi nzuri ya Israeli"

ilikuwa kubwa na matokeo yake iliinua vita

Mahali hapa pembe amepewa sifa za mtu na anajihusisha katika vita.

Baadhi ya jeshi na nyota kadhaa zilitupwa chini duniani

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. Pembe ilitupa baadhi ya jeshi na baadhi ya nyota chini ya dunia.

zilikanyagwa.

mahali hapa "pembe" imepewa sifa za binadamu na amezikanyaga nyota na juu ya jeshi.

Daniel 8:11

Alizidi kuwa mkubwa, mkubwa kama

Hapa pembe ya mbuzi inasemwa kana kwamba ilikuwa ni mtawala ambaye alifanyika mkuu.

Sadaka za kuteketezwa za kila siku ziliondolewa mbali na yeye

Neno "ziliondolewa" lina maana ya alizizuia sadaka. Pembe inaongelewa kana kwamba alikuwa ni mtawala wa kibinadamu.

sehemu yake takatifu zilitiwa unajisi

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Ilitengeneza sehemu yake takatifu kuwa najisi"

Pembe itautupa ukweli chini ardhini

Hii ina maana kwamba pembe itakataa ukweli na utauwa. Pembe inasemwa kana kwamba alikuwa ni mtawala wa kibinadamu.

Daniel 8:13

mtakatifu mmoja

"malaika"

ukabidhiajia wa sehemu takatifu

"kutiisha sehemu takatifu"

jeshi la mbinguni kukanyagwa

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "pembe ilikanyaga juu ya jeshi la mbinguni"

jioni na asubuhi zipatazo 2,300

Mahali hapa maneno "jioni na asubuhi" yanarejelea kila kitu kilicho katikati yake, iliyo na maana ya siku kamili.

mahali patakatifu patawekwa sawa.

"hekalu litasafishwa na kuwekwa katika utaratibu tena. "

Daniel 8:15

mfereji wa Ulai

Mfereji ni shimo lililotengenezwa na watu kwa ajili ya kupitisha maji.

sauti ya mtu ikiita

Mahali mtu amerejelewa kwa sauti yake. "mtu alikuwa akiita kutoka mfereji wa Ulai"

nilisujudia hadi chini

Hili ni tendo la ibada ambalo katika hilo mtu fulani hulala wima juu ya nchi.

wakati wa mwisho

"siku za mwisho" au "mwisho wa dunia" Hii hairejelei mwisho wa muda kidogo, bali matendo ambayo yatatokea ghafla kabla ya mwisho.

Daniel 8:18

usiingizi mzito

Hii ni aina ya usingizi ambao mtu hulala fofo na hawezi kuamka kiurahisi.

kipindi cha ghadhabu

Hii inarejelea wakati ambapo Mungu atahukumu.

wakati wa mwisho uliopangwa

"wakati ambapo dunia itafikia mwisho"

Daniel 8:20

Maelezo ya jumla

Katika mistari hii, malaika anamwelezea Danieli maana ya kimfano ya vitu alivyoviona katika maono yake. Wanyama na pembe kiuhalisia zinawakilisha watawala wa kibinadamu na falme.

pembe mbili ni

"pembe mbili zinawakilisha"

wafalme wa Umedi na Uajemi

Maana zinazokubalika ni 1) hii inarejelea wafalme wa Umedi na Uajemi au 2) hiki ni kiwakilishi cha falme za Umedi na Uajemi.

mfalme wa Ugiriki

Maana zinazokubalika 1) hii inarejelea mfalme wa Ugiriki au 2) hiki ni kiwakilishi cha ufalme wa Ugiriki.

Pembe kubwa katikati ya macho yake

"Pembe kubwa katikati ya macho yake inawakilisha"

Daniel 8:22

Na kuhusu pembe iliyovunjika.... pembe zingine nne zilichipuka

"mahali ambapo pembe kubwa ilivunjikia, pembe zingine nne zilizuka"

Maelezo ya jumla

Katika mistari hii, malaika anamwelezea Danieli maana ya mifano ya vitu vile alivyoona katika maono yake. Pembe kiuhalisia zinawawakilisha watawala wa kibinadamu au falme.

falme nne zitakazoinuka kutoka katika taifa lake

Pembe nne zinawakilisha falme mpya nne. Hii yaweza kuwekwa wazi. " zinawakilisha falme nne ambazo ndani yake ufalme wa mfalme wa kwanza utagawanyika."

lakini hazitakuwa na nguvu kubwa

"lakini hazitakuwa na nguvu nyingi kama mfalme aliyewakilishwa na pembe ndefu"

Katika siku zijazo za falme hizo,

Kama falme zile zilipokaribia mwisho"

watakuwa wamefikia kikomo

"wamefikia ukamilifu wao"

uso katili

Hii ina maana kwamba mtu huyo anaonekana akiwa na ukatili au mkaidi aliyekataa kutii.

Daniel 8:24

Maelezo ya jumla

Katika mistari hii, malaika anamwelezea Danieli maana ya ishara ya vitu ambavyo aliviona katika maono yake. Wanyama na pembe zinawakilisha watawala wa kibinadamu au falme.

lakini si kwa nguvu zake mwenyewe

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo chanya. "lakini mtu fulani atampa nguvu zake"

Ataufanya udanganyifu usitawi

Hapa neno "udanganyifu" unaongelewa kana kwamba alikuwa ni mtu ambaye atafanikiwa. "kiwango cha uongo utaongezeka"

chini ya mkono wake

Hapa "mkono" unarejelea utawala wake. "chini ya utawala wake."

Mfalme wa wafalme

HIi inamrejelea Mungu

akini si kwa mkono wowote wa binadamu

Neno ''mkono'' lina maana ya nguvu/mtawala.

Daniel 8:26

Maelezo ya jumla

Malaika anaendelea kumwagiza Danieli juu ya maono ambayo Danieli aliyaona.

uyafunge maono haya

Malaika anaongea juu ya maono kana kwamba lilikuwa ni gombo ambalo laweza kufungwa kwa chapa ya nta. Na hii humzui kila mtu asiweze kuona kile kilichomo mpaka pale chapa yake itakapovunjwa.

Daniel 8:27

nilichoka sana na nikalala nikiwa dhaifu kwa siku kadhaa

"alikuwa amechoka na alilala kitandani akiwa anaumwa kwa siku kadhaa"

nikaenda kufanya kazi za mfalme

"nilifanya kazi ambazo Mfalme alikuwa amenipangia"

nilikuwa nimetishwa sana na maono

"Nilikuwa nimeshangazwa na maono" au " nilichanganywa na maono"

Daniel 9

Daniel 9:1

Maelezo ya jumla

Sura ya 7 na ya 8 haziko katika mtririko wa moja kwa moja. Zilitokea wakati Belshaza alipokuwa akali ni mfalme. Sura ya 8 imeyarudia matukio ya utawala wa Dario ambaye alikuwa mfalme katika sura ya 6.

Alikuwa na Ahasuero ambaye alifanywa mfalme juu ya ufalme wa watu wa Babeli.

Haya ni maelezo ya nyuma kumhusu Ahasuero alikuwa ni nani.

ambaye alifanywa mfalme juu ya ufalme wa watu wa Babeli.

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "ambaye alikuwa mfalme juu ya Wababeli" au "ambaye aliwashinda Wababeli."

juu ya ufalme

"juu ya nchi"

kungekuwa na miaka sabini hadi mwisho wa kuachwa kwa Yerusalemu ungefika.

"tangu kipindi cha kuangushwa kwa Yerusalemu, itabaki katika hali ya ukiwa kwa miaka 70"

kuachwa

Hii ina maana ya kwamba hakuna ambaye angeweza kusaidia au kuijenga tena Yerusalemu katika kipindi kile.

Daniel 9:3

Niliugeuza uso wangu kumwelekea Bwana Mungu

Hapa "uso" unawakilisha kusudi la Danieli. "Nililielekeza kusudi langu kwa Bwana Mungu"

kumtafuta yeye

Wale wanaotaka kumjua Yahweh na kumpendeza Yeye wanasemwa kana kwamba walikuwa wakimtafuta ili kumpata Yahweh.

kufunga, na kuvaa nguo za magunia na kukaa katika majivu.

Hizi ni ishara za matendo ya toba na huzuni

niliungama dhambi zetu

"Nilikiri dhambi zetu"

hutunza maagano na uliye mwaminifu katika kuwapenda wale wanaokupenda

"hufanya kile alichokisema angelikifanya katika agano lake na hutunza ahadi zake ili kuwapenda wale"

Daniel 9:5

Maelezo ya jumla

Danieli anaendelea kumwomba Mungu juu ya watu wa Israeli.

Tumetenda dhambi na tumefanya yaliyo mabaya

Virai hivi viwili vinaelezea wazo moja katika njia mbili ili kutia mkazo.

Tumeenenda kwa uovu na tumeasi

Virai hivi viwili vinaelezea wazo moja katika njia mbili ili kutia mkazo.

amri na maagizo yako

Maneno haya "amri na maagizo" yana maana moja na yanarejelea sheria zote kwa ujumla.

Hatujawasikiliza watumishi wako

Mahali hapa "hatujawasikiliza" ina maana kwamba hawakuutii ujumbe wao.

kwa jina lako

Neno "jina" linarejea mamlaka ya Mungu. "kuzungumza kwa mamlaka"

watu wote wa nchi

Mahali hapa neno "nchi" linairejelea Israeli. "watu wa Israeli."

Daniel 9:7

Maelezo ya jumla

Danieli anaendelea kumwomba Bwana kwa ajili ya watu wa Israeli.

Kwako Bwana, kuna uadilifu

Nomino dhahania "uadilifu" yaweza kuelezwa kwa kutumia kitenzi. "Bwana, wewe unatenda kwa uadilifu"

Hata hivyo, kwetu kuna aibu katika nyuso zetu, kwa..

Nomino dhania "aibu" yaweza kuelezwa kama kitenzi. "Lakini kwetu, tumeaibika kwa ajili ya hayo ambayo tumeyatenda"

kwetu sisi

neno "sis" linamjumuisha Danile na waisraeli, lakini halimjumuishi Mungu.

kuna aibu katika nyuso

Nahau hii ina maana ya aibu yao inaonekana kwa watu wote.

kwasababu ya udanganyifu mkubwa tulioufanya

"kwa kuwa tumekusaliti wewe " au "kwasababu tumekuwa si waaminifu kwako"

Daniel 9:9

Maelezo ya jumla

Danieli anaendelea kumwomba Bwana kwa ajili ya watu wa Israeli.

Kwa Bwana Mungu wetu kuna huruma na msamaha

Kuwa na sifa hizi kunasemwa kana kwamba kumilikiwa na Bwana. "Bwana Mungu wetu ni mwenye huruma na msamaha."

Hatujaitii sauti ya Yahweh

Mahali "sauit'' inarejelea maagizo ambayo Yahweh aliyasema. "hatujatii kile ambacho Yahweh ametuambia kukifanya"

kugeukia upande,

Maneno "kugeukia upande" yana maana kwamba Israeli iliacha kuzitii sheria za Mungu.

vilivyoandikwa katika sheria ya Musa

Maneno haya yaweza kuandikwa kwa muundo tendaji. "ambavyo Musa aliyaandika katika sheria"

zimemwagwa juu yetu

Wingi wa laana na kiapo vinasemwa kana kwamba yalikuwa ni maji yamemwaga. "Umeleta juu yetu"

Daniel 9:12

Maelezo ya jumla

Danieli anaendelea kumwomba Bwana kwa ajili ya watu wa Israeli.

Kwa kuwa chini ya mbingu yote ...... na kile kilichofanyika huko Yerusalemu

Danieli anatia chumvi kuonesha huzuni yake kubwa juu ya Yerusalemu. Miji mingi imekwisha haribiwa kweli.

haijawahi kufanyika kitu chochote

"hakuna kilichofanyika"

kile kilichofanyika huko Yerusalemu

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Kile mlichokifanya katika Yerusalemu"

kama ilivyoandikwa kwenye sheria ya Musa

Muundo tendaji waweza kutumika. " Kama Musa alivyoandika katika sheria"

kugeuka na kuacha maovu yetu

Kuacha matendo mabaya kunasemwa kana kwamba ni kugeuka kutoka katika uovu. "kuacha matendo yetu mabaya"

Yahweh ameyaweka tayari maafa

"Yahweh amekwisha kuandaa majanga"

bado hatujaitii sauti yake.

mahali hapa "sauti" inarejelea mambo ambayo Yahweh alikuwa ameyaagiza. "hatujafanya yale uliyotuambia tuyafanye"

Daniel 9:15

mkono wenye nguvu

Mahali "mkono wenye nguvu" una maana ya "nguvu"

umejifanyia jina maarufu kwa ajli yako mwenyewe, hata siku hii ya leo

"umewafanya watu kujua jinsi ulivyo mkuu, kama vile ulivyo hata leo"

Lakini bado tumekutenda dhambi; tumefanya mambo ya hila

Vishazi hivi viwili kimsingi vinamaanisha kitu kimoja na vimetumika kwa pamioja kwa ajili ya kutia mkazo juu ya dhambi ilivyo mbaya.

tumekutenda dhambi; tumefanya mambo ya hila

Danieli na Waisraeli walitenda dhambi na kufanya mambo mabaya, lakini kiwakilishi "tu"hakimjumuishi Mungu.

hasira na ghadhabu yako

Maneno " hasira na ghadhabu" yana maana moja na yametumika hapa kwa ajili ya kutia mkazo juu ya hasira ya Mungu ni ya hatari inapotenda kazi"

Mlima wako mtakatifu

Mlima huu waweza kuwa mtakatifu kwasababu Hekalu la Mungu liko pale. "Mlima ambako hekalu lako takatifu liko"

dhambi zetu....baba zetu

Mahali hapa neno "zetu" linamrejelea Danieli na Israeli, lakini si kwa Mungu.

kitu cha kudharauliwa

"lengo la kutoheshimiwa"

Daniel 9:17

Basi sasa

Hii haina maana ya "wakati huu", bali ni njia ya kuonesha kwamba jambo jingine linalofuata katika maombi ya Danieli liko karibu kuanza.

mtumishi wako na maombi yake kwa ajili ya rehema;

Maneno "mtumishi wako" na "yake" yanamrejelea Danieli. Anajiongelea yeye mwenyewe katika nafsi ya tatu kama ishara ya heshima kwa Mungu.

maombi kwa ajili ya rehema

"dua kwa ya huruma"

ufanye uso wako ung'ae

Mwandishi anamwongelea Yahweh akitenda kwa neema kana kwamba Uso wa Yahweh uling'aa kwa mwanga.

sehemu yako takatifu

Inarejelea hekalu la Yerusalemu

fungua masikio yako na usikie

"kufungua masikio yako na kusikia" ni nahau yenye maana ya kusikia. Virai hivi viwili vinamaanisha kitu kile kile na kukazia hamu ya Danieli kwa Mungu ili ayasikilize maombi yake.

unaoitwa kwa jina lako

Mahali hapa "jina'' linawakilisha umiliki. "ni mali yako"

usichelewe

Hii yaweza kuelezwa kwa sentensi chanya. "fanya haraka"

Daniel 9:20

watu wangu

"watu wa Israeli ambako mimi ninatokea"

Mlima mtakatifu wa Mungu

Mlima waweza kuwa mtakatifu kwasababu ya hekalu. "mlima ambako kuna hekalu takatifu la Mungu"

mtu Gabrieli

Huy ni Gabrieli yule yule ambaye alionekana katika umbo la Mwanadamu katika 8:15

katika ndoto hapo awali,

Hii yaweza kurejelea maono ya mwanzo ambayo Danieli aliyaona wakati alipokuwa macho.

alipaa kwa kasi kushuka kuja nilipo

"alipaa haraka akija nilipo"

wakati wa sadaka ya jioni

Watu wa Kiyahudi walitoa sadaka kila jioni kabla jua halijazama.

Daniel 9:22

utambuzi na ufahamu

Maneno "utambuzi na ufahamu" yanamaanisha kitu kile kile na yanatia mkazo kwamba Gabrieli atamsaidia Danieli kuuelewa ujumbe.

amri ilitolewa

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Mungu alitoa amri"

tafakari neno hili

Mahali hapa "neno" linarejelea ujumbe wote. "firikiria juu ya ujumbe huu"

ufunuo

Hii inarejea nyuma kwa unabii wa Yeremia katika 9:1

Daniel 9:24

Miaka sabini na saba zimeamriwa kwa ajili ya watu wako na mji wako mtakatifu

Mungu alitoa amri kwamba angefanya mambo kwa ajli ya watu na mji mtakatifu

Miaka sabini na saba...majuma saba na majuma sitini na mbili.

Hii si njia ya kawaida ya kuhesabu kwa Waisraeli. Kama itawezekana tafsiri kwa njia ambayo itatunza matumizi ya namba saba. "sabini mara miaka saba...saba mara miaka saba... sitini na mbila mara miaka saba"

watu wako na mji wako mtakatifu

Neno "wako" linamrejelea Danieli. Watu ni Waisraeli na mji mtakatifu ni Yerusalemu.

kukomesha hatia na kumaliza dhambi

Wazo limerudiwa ili kutia mkazo juu ya jinsi jambo hili litakavyotokea.

kutimiza maono

Hapa maneno 'kutimiza maono" ni nahau yenye maana ya kuhitimisha. "kukamilisha maono"

maono na unabii

Maneno haya katika muktadha huu yana maana moja. Yanatoa uhakika kwa Danieli kwamba maono ya Yeremia yalikuwa ni unabii kweli.

Ujue na kufahamu

Maneno haya yametumika kwa pamoja kuonesha na kuufanya umuhimu uwe wazi.

Mpakwa mafuta

Kutia mafuta ni tendo la ishara linaloonesha kwamba mtu fulani alichaguliwa. "Mtu yule ambaye Mungu anamtia mafuta"

kutakuwa na majuma saba na majuma sitini na mbili.

Haya yakiwekwa pamoja ni 69 kati ya 70 saba ilivyoongelewa ni 24.

Yerusalemu itajengwa

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "watu wataijenga Yerusalemu"

handaki

ni shimo chini ya ardhi kuuzunguka mji au jengo, mara kwa mara huwa na maji ndani yake.

kwa nyakati za shida

"muda wa mateso makubwa"

Daniel 9:26

sitini na mbili saba

Hii si njia ya kawaida ya kuhesabu kwa Waisraeli. Kama inawezekana jaribu kuhifadhi matumizi ya namba saba.

mtiwa mafuta ataharibiwa na atakuwa hana kitu chochote

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "watu watamharibu mpakwa mafuta na hatakuwa na kitu"

mpakwa mafuta

kupaka mafuta ni tendo la ishara linaloonesha kwamba mtu fulani amechaguliwa.

kiongozi ajaye

Huyu ni mtawala wa kigeni, si "mpakwa mafuta"

Mwisho wake utatatokea kwa gharika,

Jeshi litauharibu mku na sehemu takatifu kama vila gharika linavyoharibu vitu.

Uharibifu umekwisha amriwa.

Kauli hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Mungu amekwisha amuru kuuharibu mji na mahali patakatifu."

Daniel 9:27

Ata....ata...

Hii inamrejelea mtawala akayekuja ambaye atamharibu mpakwa mafuta.

miaka saba...Katikati ya miaka saba

Mahali neno "saba" limetumika kurejelea kipindi cha miaka saba.

atakomesha

"kuacha" au "kusimamisha"

dhabihu na sadaka

maneno haya kimsingi yanamaanisha kitu kile kile. Marudio yanaonesha kwamba mtawala ajayea atakomesha aina zote za sadaka.

mtu atakayeleta ukiwa

Mtu ambaye atateketeza kabisa"

Mwisho kamili na uharibifu umeamriwa kutokea kwa yeye aliyesababisha ukiwa.

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Mungu ameamuru kwamba ataleta mwisho kamili na uharibifu"

Mwisho kamili na uharibifu

Maneno haya mawili yana maana moja. Yanatia mkazo juu ya uhalali na ukamilifu wa uharibifu.

yeye aliyesababisha ukiwa

"mtu ambaye ataleta uharibifu"

Daniel 10

Daniel 10:1

Katika mwaka wa tatu wa Koreshi mfalme

"mwaka wa 3 wa utawala wa Koreshi mfalme"

ujumbe ulifunuliwa kwa Danieli

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Mungu aliufunua ujumbe kwa Danieli"

ufumbuzi

"ufahamu"

Daniel 10:2

Sikula chakula kizuri

Hakuna chakula cha gharama kubwa au chakula adimu

mpaka ukamilifu wa wiki tatu nzim

"hadi mwisho wa majuma matatu mazima"

Daniel 10:4

4Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kwanza,

Huu ni mwezi wa kwanza wa kalenda ya Kiebrania. Siku ya ishirini na nne iko karibu na katikati ya mwezi wa Aprili matika kalenda ya Magharibi.

akiwa na mkanda kiunoni mwake

"na alikuwa amevaa mkanda"

Ufazi

Ufazi ni sehemu. sehemu yake haijulikanai.

Mwili wake ulikuwa kama kito

Mwlii wake uling'ara kwa mwanga wa bluu na njano kana kwamba ulikuwa umetengenezwa kwa kito.

kito

jiwe la thamani lenye rangi ya bluu au njano.

na sura yake ilikuwa kama radi

Sura yake iling'aa kama mwali wa radi unavyong'ara.

Macho yake yalikuwa kama miali ya tochi

Macho yake yalikuwa yanang'aa kwa mwanga kana kwamba yalikuwa miali ya tochi.

mikono yake na miguu yake ilikuwa kama shaba iliyosafishwa

Mikono yake na miguu yake ilikuwa iking'aa kana kwamba ilikuwa imetengenezwa kwa shaba iliyosafishwa.

Sauti ya maneno yake ilikuwa kama sauti ya umati mkubwa wa watu

Sauti yake ilikuwa na nguvu sana kwamba ilikuwa ni kundi kubwa la watu wengi likiongea kwa sauti ya juu.

Daniel 10:7

Hivyo niliachwa peke yangu

"Hakuna yeyote aliyekuwa pamoja nami, na niliona"

mwonekano wangu wa kung'aa ulibadilika na kuwa mwonekano wa uharibifu

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "mwonekano wangu unaong'aa ulibadilika kuwa katika mwonekano ulioharibiwa"

mwonekano wangu wa kung'aa

Hii inaelezea juu ya uso wa mtu fulani ambaye ana afya nzuri.

Mwonekano ulioharibiwa

Uso mbaya, usio na afya na wa kikatili unasemwa kana kwamba ni jengo.

Nilisikia maneno yake

Hii ina maana kwamba mtu fulani alikuwa anazungumza katika maono. Hii yaweza kuwekwa wazi. "Nilisikia maneno ya mtu aliyekuwa anaongea"

nilianguka kifudifudi na kupata usingizi mzito

Danieli aliogopeshwa na kile alichokiona na ya kwamba huenda alilala chini ardhini, mahali ambapo alizimia.

Daniel 10:10

Mkono ulinigusa

Hii ni lugha ya picha inayowakilisha mtu, huenda ni mtu yule ambaye Danieli alimwona.

Danieli, mtu aliyetunzwa

Hii pia yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji."Danieli, wewe ambaye Mungu anakuhifadhi sana"

aliyetunzwa sana

anayethaminiwa na kupendwa sana

Daniel 10:12

ulipoiweka akili yako kutaka kufahamu

"ulihitaji kufahamu maono"

maneno yako yalisikiwa

Kauli hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Mungu aliyasikia maneno yako"

Mwana wa mfalme

hii inarejelea roho ambayo ina mamlaka juu ya taifa la mtu.

mfalme wa Uajemi

Hii huenda inarejelea wafalme mbalimbali waliotawala mataifa mbalimbali katika dola ya Uajemi, na wale waliopaswa kumtii mfalme wa Uajemi.

Daniel 10:14

Maelezo ya jumla

Malaika anaendelea kuongea na Danieli

niligeuza uso wangu na kuuelekeza chini

"Niliangalia chini ardhini" Danieli huenda alifanya hivi ili kuonesha unyenyekevu katika heshima kubwa, au kwasababu alikuwa ameogopa.

Daniel 10:16

Yeye aliyekuwa kama wana wa mtu

Kauli hii inamrejelea yeye ambaye alikuwa ameongea na Danieli. Ingawa, baadhi ya matoleo hutafsiri kwamba alikuwa anamrejelea mtu mwingine tofauti.

kama wana wa mtu

Maelezo haya yanawarejelea watu kwa ujumla

masumbuko

mateso makali ya kihisia

Mimi ni mtumishi wako. Je ninawezaje kuongea na Bwana wangu?

Danieli anauliza swali hili kumaanisha kwamba yeye hawezi kuongea na malaika kwasababu yeye halingani na malaika. Sentensi hizi zaweza kuunganishwa. "siwezi kukujibu wewe kwasababu mimi ni mtumishi wako"

hakuna pumzi iliyosalia ndani yangu."

Nahau hii inarejelea upumuaji. "Siwezi kupumua" au "ni vigumu sana kupumua"

Daniel 10:18

ule mwenye mwonekano wa mtu

"Yeye anayeonekana kama mtu"

Uwe mwenye nguvu, uwe na nguvu

Maneno "Uwe mwenye nguvu" yamerudiwa kwa ajili ya kutia mkazo.

mtu ulithaminiwa sana

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "wewe ambaye Mungu amekuthamini sana"

umenitia nguvu

Kauli hii pia yaweza kuandikwa kwa muundo tendaji."Nilikuwa mwenye nguvu"

Daniel 10:20

mkuu wa Uajemi

"mkuu" hurejelea roho ambayo inatawala na kulilinda taifa la watu. "mkuu wa roho ya uajemi"

Lakini nitakwambia

Hii ina maana kwamba Malaika atamwambia Danieli juu ya hili muda mfupi kabla hajaenda mbali.

kile kilichoandikwa katika Kitabu cha Ukweli

Kauli hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "kile Kitabu cha Ukweli kinayasema" au "kile ambacho mtu fulani alikiandika katika Kitabu cha Ukweli.

yeyote anayejionesha kuwa na nguvu

"yeye anayejihakikisha kuwa na nguvu"

isipokuwa Mikaeli mkuu wenu

Kirai hiki chaweza kuelezeka kama sentensi inayojitegemea. "Mikaeli mkuu wako ni yeye pekee ambaye huyatenda haya"

Mikaeli mkuu wenu

Neno "wenu" liko katika wingi. Linamrejelea Danieli na watu wengine waliosalia wa Israeli.

Mkuu

Angalia jinsi ulivyotafsiri "mkuu" inapomrejelea Mikaeli katika 10:12.

Daniel 11

Daniel 11:1

Maelezo ya jumla

Katika Danieli 11:1 hadi 12:4, yeye aliyekuwa akiongea na Danieli katika sura ya 10 anamwambia kile kilichoandikwa katika kitabu cha ukweli. Hiki ni kama kile alichosema angekifanya katika 10:20.

Katika mwaka wa kwanza wa Dario

Dario alikuwa ni Mfalme wa Umedi. "Mwaka wa kwanza" hurejelea mwaka wa kwanza ambao alikuwa Mfalme.

Wafalme watatu watainuka katika Uajemi,

"Wafalme watatu watatawala juu ya Uajemi"

na mfalme wa nne atakuwa tajiri sana kuliko wengine wote

"baada yao mfalme wa nne atakuja kutawala ambaye atakuwa na fedha nyingi kuliko watatu waliomtangulia"

nguvu

Maana zinazoweza kukubalika ni 1)mamlaka au 2) nguvu za kijeshi

atamwamsha kila mtu

"atamsababisha kila mtu atake kupigana"

Daniel 11:3

Maelezo ya jumla

Malaika anaendelea kuongea na Danieli.

Mfalme wenye nguvu atainuka

Wazo la kusimama au kuinuka mara kwa mara limetumika kwa ajili ya mtu anayekuwa na nguvu.

ambaye atatawala ufalme mkubwa

Maana zinazokubalika ni 1)ukubwa wa ufalme huu utakuwa wa ajabu, au 2) kwamba mfalme angetawala ufalme wake kwa nguu kubwa.

falme wake utavunjika na utagawanyika

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "ufalme wake utavunjika na kugawanyika" au "ufalme wake utavunjika katika vipande vipande"

pepo nne za mbinguni

Angalia jinsi ulivyofasiri 7:1

lakini hawatakuwa wazao wake mwenyewe,

Wazo la kutokugawanywa linamaanishwa hapa. "Lakini hautagawanywa kwa watoto wake mwenyewe"

falme wake utang'olewa kwa ajili ya wengine tofauti na wazawa wake

Ufalme unaongelewa kana kwamba ni mmea ambao mtu fulani anaweza kuuharibu kwa kuung'oa. Wazo hili laweza kuelezeka kwa muundo tendaji. "utawala mwingine utaung'oa na kuuharibu ufalme wake, na watu wengine ambao siyo watoto wake watautawala.

Daniel 11:5

Maelezo ya jumla

Malaika anaendelea kuongea na Danieli

mmoja kati ya maamiri jeshi wake atakuwa mwenye nguvu kuliko yeye na atautawala ufalme wake kwa nguvu kubwa

Kamanda wa mfalme wa Kusini atakuwa Mfalme wa Kaskazini.

watafanya mwungano

Mfalme wa Kusini atafanya ushirika na Mfalme wa Kaskazini. Mwungano huu utakuwa wa makubaliano rasmi ambayo kila taifa lazima kuyafuata.

Binti wa mfalme wa Kusini atakuja kwa mfalme wa Kaskazini kuyathibitisha makubaliano yao.

Mfalme wa Kusini atampa binti yake mfalme wa kusini ili amwoe. Ndoa itathibitisha makubaliano kati ya wafalme hawa wawili.

nguvu za mkono wake.... mkono wake

Mahali hapa "mkono" unatumika kumaanisha nguvu.

Ataachwa

Hii inarejelea hila ya kuuliwa kwa binti na wale ambao wamefanya mwungano. Kirai hiki chaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. " Watamwacha"

Daniel 11:7

Maelezo ya jumla

Malaika anaendelea kuongea na Danieli

tawi kutoka katika mizizi

Familia inaongelea kana kwamba ni mti. Mizizi inawakilisha mababu, na matawi yanawakilisha wazawa.

mizizi yake

Neno "yake" inarejelea kwa binti wa mfalme wa Kusini katika 11:5

Atalishambulia jeshi

Kiwakilishi "a" kinarejelea uzao wake, na hapa pia inawakilisha jeshi lake.

Atapigana nao

Mahali hapa neno "nao" inawakilisha wanajeshi wa jeshi la adui.

lakini atajitoa

Kiambishi 'a' kinamrejelea mfalme wa Kaskazini.

Daniel 11:10

Maelezo ya jumla

Malaika anaendelea kuongea na Danieli

Wana wake

"wana wa mfalme wa Kaskazini"

kuunganisha jeshi kubwa

"kukusanya watu wengi kwa pamoja ambao wanaweza kupigana katika vita"

litagharikisha kila kitu

Kitendo cha jeshi kubwa kuivamia na kuijaza nchi yote kitakuwa sawa na maji ya gharika.

Daniel 11:11

Maelezo ya jumla

Malaika anaendelea kuongea na Danieli.

atainua jeshi kubwa

"atakusanya jeshi kubwa"

jeshi litatiwa katika mkono wake

Mahali hapa neno "mkono" linawakilisha utawala wa mfalme

Jeshi litachukuliwa

Hii yaweza kuandikwa kwa muundo tendaji. "Mfalme wa Kusini ataliteka jeshi la Kaskazini"

utainuliwa juu

Kuinuliwa juu kunawakilisha wazo wa kuwa na kiburi.

atawafanya makumi maelfu kuanguka

Mahali hapa kuanguka kunawakilisha kufa katika vita.

makumi maelfu

"Maelfu mengi"

Daniel 11:13

Maelezo ya jumla

Malaika anaendelea kuongea na Danieli.

jeshi kubwa likiwa na vifaa vingi

Hii pia yaweza kuandikwa kwa muundo tendaji. "jeshi kubwa ambalo litakua na zana za kutosha"

Daniel 11:14

Maelezo ya jumla

Malaika anaendelea kuongea na Danieli.

wengi watainuka kinyume na mfalme

Mahali hapa wazo la kuinuka linawakilisha uasi. "watu wengi wataasi kinyume na mfalme"

Wana wa vurugu

Maelezo haya yanasimama kwa ajili ya watu wenye vurugu

watajikwaa

Mahali hapa kitendo cha kujikwaa kinamaanisha kuanguka.

Daniel 11:15

Maelezo ya jumla

Malaika anaendelea kuongea na Danieli.

Mfalme wa Kaskazini atakuja

Hapa "mfalme wa Kaskazini" anajumuisha na jeshi lake pia. "Jeshi la mfalmw wa Kaskazini litakuja"

kuizingira nchi kwa kuweka vilima

Hii inarejelea kitendo cha kurundika udongo ili wanajeshi waweza kuufikia urefu wa ukuta wa mji iili kuwashambulia. Wanajeshi na watumwa wataweka udongo kwenye vikapu na kuvibeba hadi mahali sahihi, na kuumwaga ili kuinua kilima cha udongo.

Mfalme wa Kaskazini atakuja, kuizingira nchi kwa kuweka vilima

"Mfalme wa Kaskazini" hapa inamaanisha wanajeshi katika jeshi la mfalme, ambao wangefanya kazi halisi ya kutengeneza vilima vya udongo.

ngome

Kuta na vitu vingine vilivyojengwa ili kulinda mji

Hawatakuwa na nguvu za kusimama

Mahali hapa kitendo cha kusimama kinawakilisha uwezo wa kupigana.

yeye ajaye ataenenda kwa kufuata tamaa zake kinyume chake

"Mfalme atakayevamia atafanya kili kitu anachokitaka kinyume na mfalme mwingine."

Atasimama

Mahali hapa kusimama kuna maana ya kutawala

nchi ya uzuri

Hii inarejelea nchi ya Israeli . angalia ulivyotafsiri katika 8:9

uharibifu utakuwa mkononi wake

Mahali hapa "uharibifu" unawakilisha nguvu ya kuharibu. Pia, nguvu ya kuharibu inasemwa kana kwamba kilikuwa ni kitu ambacho mtu anaweza kukishikilia katika mikono yake.

Daniel 11:17

Maelezo ya jumla

Malaika anaendelea kuongea na Danieli

atauelekeza uso wake

"kuamua"

kuja kwa nguvu

Hii huenda inarejelea juu ya nguvu za kivita.

binti wa wanawake

Hii ni njia ya madaha ya kusema "mwanamke"

atakikomesha kiburi chake

"atamfanya mfalme wa Kaskazini asiwe na atakisababisha kiburi chake kiishekiburi"

atakisababisha kiburi chake kiishe

"atamsababisha mfalme wa Kusini ateseke kwasababu alikuwa na kiburi dhidi ya wengine"

atafuatilia

"Mfalme wa Kaskazini atazingatia"

hatapatikana

Hii ni njia ya kusema kuwa atakufa. Wazo hili laweza kuandikwa kwa muundo tendaji. "atatoweka" au "atakufa"

Daniel 11:20

mtu mwingine atainuka

Kuinuka katika nafasi ya mfalme inawakilisha kufanyika kuwa mfalme katika nafasiya mfalme aliyepita.

atamfanya mtoza ushuru apite

mtoza ushuru atapita katika nchi akiwalazimisha watu walipe kodi.

atakatiliwa mbali

Kiambishi 'a' kinamrejelea mfalme mpya. Kukatiliwa mbali ina maana ya kufa.

lakini si kwa hasira

Maana zinazokubalika 1) hakuna hata mmoja aliyekuwa na hasira na mfalme 2) tuko hilo na sababu ya kifo cha mfalme yalitunzwa kama siri.

mtu wa kudharauliwa ambaye watu hawatampa heshima ya nguvu ya kifalme

Watu watakataa kumheshimu kama mfalme kwasababu yeye si mzawa wa wafalme.

jeshi litafutiliwa mbali kama gharika

Kufutiliwa mbali kunawakilisha hali ya kuharibiwa. Hii pia yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji."jeshi lake litaangamiza kabisa jeshi kubwa kama gharika linavyoteketeza kila kitu katika njia yake"

Jeshi na kiongozi wa agano wataangamizwa wote kwa pamoja

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "ataliangamiza jeshi na kiongozi wa agano"

kiongozi wa agano

Kirai hiki kinamrejelea mtu alijawa na nafasi muhimu ya kidin ambayo Mungu anaihitaji katika agano, ambaye ni kuhani mkuu (ambaye aliuawa katika mwama 171 KK)

Daniel 11:23

Tangu katika kipindi kile ambacho makubaliano yalifanywa pamoja naye

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "wakati viongozi wengine walipofanya mkataba wa amani pamoja naye"

Atagawanya mateka, nyara, na mali zake miongoni mwa wafuasi wake

"atagawa kwa wafuasi wake"

mateka, nyara, na mali

"vitu vya thamani ambaye yeye na jeshi lake walichkua kutoka kwa watu waliowashinda"

Daniel 11:25

Ataamsha nguvu zake na moyo wake

Nguvu na moyo (ni ujasiri) vinaongelewa kana kwamba walikuwa ni watu ambao mtu fulani angeweza kuwaamsha ili watendo tendo.

moyo

Mahali hapa unawakilisha ujasiri

atapigana vita

"atapigana kinyume chake"

jeshi kubwa

"pamoja na jeshi kubwa ambalo atalikusanya"

hataweza kusimama

Kutokusimama kunawakilisha hali ya kushindwa.

wanaokula chakula chake kizuri

Hii inarejelea washauri wa mfalme. Ilikuwa na kawaida kwa washauri waliominiwa na mfalme kula chakula pamoja naye.

jeshi lake litakatiliwa mbali kama gharika,

Mahali hapa kushindwa kabisa kwa jeshi kunasemwa kana kwamba lilikuwa ni gharika la maji ambalo hulifutilia mbali.

wengi wao watauawa

Hii inarejelea kufa katika vita.

wakiwa na mioyo yao imejawa na uovu kinyume na mwenzake

Mahali hapa neno "moyo" linawakilisha tamaa za mtu. Tamaa zinaongelewa kana kwamba kilikuwa ni kitu ambacho mtu anaweza kukiweka katika mkao fulani.

watakaa katika meza moja

Kukaa katika meza moja kuna maanisha kitendo cha kuongea pamoja na mtu mwingine.

haitakuwa na maana yoyote

"lakini mazungumzo yao hayatawasaidia"

Kwa kuwa mwisho utatokea katika kipindi ambacho kimeshapangwa

Hii inatuambia kwamba mkutano wao hautakuwa na mafanikio.

Daniel 11:28

moyo wake ukipinga vikali agano takatifu

Hii inarejelea tamaa ya mfalme ya kupinga agano la Mungu na waisraeli. Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Atafahamika kwa kupinga agano takatifu."

moyo

Hii inarejelea tamaa za mfalme

agano la takatifu

Mahali hapa "takatifu" inaelezea juu ya agano la Mungu na Israeli. Ina maana kwamba agano lazoma liheshimiwe na liheshimiwe kwasababu linatoka kwa Mungu mwenyewe.

ukipinga vikali agano takatifu

Hamu ya mfalme kutenda kinyume na agano takatifu inawakilisha hamu yake kuwazuia waisraeli waache kulitii agano takatifu.

atatenda

Hii ina maana kwamba mfalme atafanya matendo fulani katika Israeli.

Daniel 11:29

meli kutoka Kitimu zitamshambulia

Meli zinawakilisha jeshi likitoka katika meli hizo.

Kitimu

Hii inarejelea makazi katika kisiwa cha Kipro katika Bahari ya Meditraniani.

Atakuwa mwenye hasira

"atakasirika sana"

atawaonyesha mema wale

"atatenda kwa wema kwa wale" au "atawasaidia wale"

Daniel 11:31

Majeshi yake yatainuka

"Jeshi lake litatokea" au "jeshi lake litakuja" Neno "lake" linamrejelea mfalme wa Kaskazini.

sehemu takatifu katika ngome

"sehemu takatifu ambayo watu huitumia kama ngome"

Wataziondoa sadaka za kawaida

Kuondolewa kwa sadaka kunawakilisha kuwazuia watu wasitoe sadaka. "Watawazuia makuhani wasitoe sadaka za kawaida za kuteketezwa"

chukizo la uharibifu litakalosababisha ukiwa.

Hii inarejelea sanamu ambayo italifanya hekalu kuwa ukiwa, hii ina maana kwamba itamfanya Mungu aliache hekalu lake.

walioenenda kwa ouvu kinyume na agano

"waliliasi agano kwa kutenda uovu"

kuwatia uovu

"kuwashawishi watende dhambi"

wale wanaomjua Mungu wao

Mahali hapa neno "kujua" lina maana ya "kuwa mwaminifu,"

watakuwa jasiri na watachukua hatua.

"watakuwa imara na kuwapinga"

Daniel 11:33

watajikwaa

Mahali hapa " kujikwaa" inawakilisha kupatwa na majanga ya aina hii au nyingine, ikijumuisha na kifo chenyewe.

Upanga

Mahali hapa "upanga"unawakilisha mapigano na vita.

miali ya moto

Mahali hapa "miali" inawakilisha moto.

watatiwa mateka

"kufanywa kuwa mtumwa"

kunyang'anywa

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Maadui zao watawaibia mali zao"

watasaidiwa kwa msaada kidogo

Hii yaweza kuwekwa katika muundo tendaji. " watu wengine watampa msaada kidogo"

Watu wengi watajiunga nao wenyewe katika unafiki

Hii inarejelea watu wengine ambao watajifanya kuwasaidia watu wenye hekima, lakini si kwasababu wamekusudia kuwasaidia kweli.

watajiunga nao

Mahali hapa "watajiunga nao" ina maana ya "kuja na kuwasaidia"

ili kujisafisha kutokee kwao,

Neno "ili" lina maana kwamba "matokeo kwamba"

Baadhi ya watu wenye hekima watajikwaa

Mahali hapa " kujikwaa" inawakilisha kupatwa na majanga ya aina hii au nyingine, ikijumuisha na kifo chenyewe

kujisafisha kutokee kwao, na kujiosha, na kujitakasa

Matendo haya yanaelezwa hapa kana kwamba ilikuwa ni vitu. Ingawa, yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji au tendewa. "watasafishwa, kuoshwa na kutakaswa"

kujisafisha

Hii inarejelea kusafisha kito kwa kukiyeyusha katika moto. Wakati Mungu anawatengeneza watu wake ili wawe waaminifu kwake, kunasemwa kana kwamba walikuwa ni vito ambavyo mfanyakazi alikuwa akivifanya kuwa safi zaidi kwa kuviweka katika moto.

kujiosha,

Hii inarejelea kitendo cha kuwatengeneza watu, sehemu au vitu ili vifae kwa ajili ya Mungu kwa kuvitenga na dhambi au aina nyingine yoyote ya ubaya. Uovu unasemwa kana kwamba ni uchafu wa kawaida.

kujitakasa,

Hili wazo ni sawa na kujisafisha, lililojadiliwa awali. Kito kilichosafishwa chaweza kusemwa kwamba chaweza kutakaswa.

wakati wa mwisho.

"siku za mwisho" au " mwisho wa ulimwengu.

Kwa kuwa wakati ulioamriwa haujaja bado

Mahali hapa 'wakati ulioamriwa' ina maana kwamba Mungu amepanga muda. Maneno haya yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Yahweh amepanga muda kwa wakati ujao"

Daniel 11:36

Mfalme atafanya kutokana na matakwa yake

Mfalme atafanya chochote akitakacho"

Mfalme

Hii inamrejelea mfalme wa Kaskazini.

Atajiinua mwenyewe na kujifanya mkubwa

Kirai "Atajiinua mwenyewe" na "kujifanya kuwa mkubwa" vina maana sawa na vinaonesha kwamba mfalme atakuwa na kiburi.

Atajiinua mwenyewe

Mahali ina maana ya kuwa na kiburi.

kujifanya mkubwa

Hapa ina maana ya kujifanya kuwa mtu wa muhimu na mwenye nguvu.

atasema vitu vibaya

"vitu vya ajabu" au "vitu ya kusikitisha"

mpaka pale ghadhabu itakapokuwa imekamilika

Kirai hiki kinaonesha picha kwamba Mungu huhifadhi ghadhabu mpaka pale stoo yake itakapokuwa imejaa na kisha atakuwa tayari sawasawa na hasira hiyo.

Mungu wa miungu

Hii inamrejelea Mungu mmoja na wa kweli. "Mungu mkuu" au "Mungu pekee wa kweli"

mungu anayependwa na wanawake

Hii inaonekana kurejelea mungu wa kipagani aliyeitwa Tamuzi.

Daniel 11:38

mungu wa ngome

Huenda mfalme aliamini kwamba huyu mungu wa uongo angemsaidia kuzishambulia ngome za watu wengine na kuitunza ngome yake.

badala ya haya

Neno "haya" linarejelea miungu iliyotajwa

ataigawanya nchi kama thawabu

Maana zinazokubalika ni 1)"atawapa wafuasi wake nchi kama thawabu au 2) ataiuza nchi kwa wafuasi wake.

Daniel 11:40

wakati wa mwisho

"siku za mwisho" au " mwisho wa ulimwengu"

mfalme wa Kusini ...... Mfalme wa Kaskazini

Virai hivi vimesimama hapa kuwakilisha wafalme na majeshi yao.

atamshambulia

Hili ni shambulio la vurugu la jeshi linasemwa kana kwamba ni dhoruba imetokea.

kuwagharikisha

Kitendo cha jeshi kusambaa katika nchi kunasemwa kana kwamba ni gharika limetokea.

kupita katikati

jeshi hitazuiliwaa na chochote.

nchi ya uzuri,

Hii inarejelea nchi ya Israeli.

wataanguka

Mahali hapa kuanguka kuna maana ya kitendo cha kufa.

Lakini watu hawa watatoroka kutoka katika mkono wake

Mahali hapa "mkono" una maana ya nguvu. "Lakini watu hawa watatoroka kutoka katika nguvu zake"

Daniel 11:42

Maelezo ya jumla

Hii bado inamhusu mfalme wa Kaskazini.

Naye ataunyosha mkono katika nchi

Mahali hapa "mkono" unawakilisha nguvu na utawala.

Katika nchi

Hapa wazo ni kwamba nchi nyingi au nchi kadhaa

nchi ya Misri haitaokolewa

Hii yaweza kuwekwa katika muundo tendaji. ""Nchi ya Misri haitatoroka"

watu wa Libya na Ethiopia watakuwa chini katika nyayo za miguu yake

Hapa " nyayo za miguu" inawakilisha hali ya kujishusha/ utii. "watu wa Libya na Ethiopia watamtumikia"

watu wa Libya na Ethiopia

"watu waLIbya na Ethiopia" Libya ni nchi ya Magharibi mwa Misri, na Ethiopia ni nchi iliyo Kusini mwa Misri.

Daniel 11:44

Maelezo ya jumla

Hii bado inamhusu mfalme wa Kaskazini.

naye atatoka akiwa mwenye hasira nyingi

Nomino dhahania "hasira" yaweza kuelezwa kwa neno "ghadhabu" Yaweza kuelezwa wazi kwamba ataenda nje pamoja na jeshi lake.

atatoka

Hapa inawakilisha kitendo cha kuwashambulia maadui.

na kuwahifadhi kwa ajli ya uharibifu

"Kuwaharibu watu wengi"

hema ya makao yake

Hii inarejelea hema za starehe za mfalme ambazo aliishi ndani yake wakati alipokuwa pamoja na jeshi lake katika wakati wa vita.

milima ya uzuri wa utakatifu

Hii inarejelea mlima wa Yerusalemu mahali ambapo hekalu la Mungu lilikuwa.

Daniel 12

Daniel 12:1

Maelezo ya jumla

Malaika anaendelea kumwagiza Danieli. Alianza katika 10:20

Mikaeli, jemedari mkuu

Mikaeli ni malaika mkuu. Mahali hapa pia amepewa jina jingine "jemedari mkuu"

watu wako wataokolewa

Mungu alifanya kitendo cha kuwaokoa watu. " Mungu ataokoa watu wako"

yeyote ambaye jina lake litapatikana katika kitabu

Mungu hufanya kazi ya kuandika katika kitabu. "wale ambao majina yao Mungu ameyaandika katika kitabu"

watu wako wataokolewa

Hii inarejelea tukio kubwa la kiroho ambapo watu wa Mungu watapewa maisha mapya, wote walio hai na walio kufa, na watu waovu watakatiliwa mbali katika hukumu ya milele.

Daniel 12:3

watang'ara kama mng'ao wa anga la juu,

Hii inawarejelea watu wa Mungu wakiwa wamejawa na utukufu wake kwahiyo watang'aa kama anga wakati juu likiwa linaangaza.

wale wenye kuwaelekeza wengine katika haki

Wale ambao huwasaidia wengine kuelewa kwamba wametengwa na Mungu wanasemwa kana kwamba walikuwa wanabadili mwelekeo walikuwa wakielekea. "ambaye huwafundisha wengine waishi katika haki"

watakuwa kama nyota milele na milele

Watu hawa watang'aa kama nyote. Hii ni tabia ya watu waliojawa na utukufu wa Mungu.

yafunge maneno haya; kihifadhi kitabu kikiwa kimetiwa chapa

Kuna mambo ambayo Danieli alikuwa ameoneshwa na kufunzwa na ya kwamba Danieli alikuwa ameambiwa kwamba asiyafunue katika kitabu hiki.

nyakati za mwisho

"siku za mwisho" au "mwisho wa ulimwengu"

Watu wengi watakimbia huku na kule, na maarifa yataongezeka.

Mambo haya yanaonekana kutokea wakati wa kufungwa kwa kitabu. Hii yaweza kuwekwa wazi. "Kabla ya kutokea haya, watu wengi watasafiri hapa na kule, wakijifunza mengi na mengi zaidi kuhusu vitu vingi"

Daniel 12:5

Maelezo ya jumla

Malaika amemaliza kuongea, na Danieli anaendelea kusema kile alichokiona baadaye katika maono yake tangu katika 10:4

kulikuwa na malaika wengine wawili wamesimama

"kulikuwa na malaika wengine wawili wamesimama"

Mmoja wao alimwambia mtu aliyevaa nguo za kitani,

Hii inamrejelea mtu aliyekuwa akiongea na Danieli, siyo mmoja wale watu waliokuwa wamesimama pembeni mwa mtu.

ukingo wa mto,

Maana zinazoweza kukubalika 1) malaika alikuwa juu ya mto au 2) malaika alikuwa mbali katika ukingo sambamba na mto.

Je itachukua muda gani mpaka mwisho wa matukio haya ya kushangaza?

"Matukio haya ya kushangaza yatadumu kwa muda gani?" Hii inarejelea mwanzo hadi mwisho wa matukio.

matukio haya ya kushangaza

Katika muda ule ambao malaika alikuwa akiongea na Danieli, hakuna hata tukio hata moja lilikuwa limetokea. Hii kwa uhalisia inarejelea matukio katika 12:1, na huenda yalijumuisha matukio yaliyo katika maono kutoka sura ya 11.

Daniel 12:7

mtu yule aliyevaa nguo za kitani

Hii yaweza kuelezwa katika muundo tendaji. " mtu aliyekuwa amevaa nguo za kitani"

mkondo wa mto

Maana zinazoweza kukubalika 1) malaika alikuwa juu ya mto au 2) malaika alikuwa mbali katika ukingo sambamba na mto.

yeye aishiye milele

"Mungu ambaye anaishi milele"

itakuwa kwa wakati, nyakati, na nusu wakati

Ni vizuri kuiacha katika utata kama ilivyoanza. Na kama utachagua sehemu ya kuanzia, miaka mitatu na nusu huenda itaanza pamoja na matukio ya 12:1.

wakati, nyakati, na nusu wakati

"miaka mitatu na nusu: Maneno "nyakati au wakati" kwa ujumla yanapaswa kufahamika kuwa yanarejelea miaka. Mwaka mmoja na miwili na nusu ni sawa na miaka mitatu na nusu.

mambo haya yote yatakuwa yamemalizika

Hii yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Mambo haya yote yatatokea"

Mambo haya yote

Katika muda ule ambao malaika alikuwa akiongea na Danieli, hakuna hata tukio hata moja lilikuwa limetokea. Hii kwa uhalisia inarejelea matukio katika 12:1, na huenda yalijumuisha matukio yaliyo katika maono kutoka sura ya 11.

Daniel 12:8

Mambo haya yote

Katika muda ule ambao malaika alikuwa akiongea na Danieli, hakuna hata tukio hata moja lilikuwa limetokea. Hii kwa uhalisia inarejelea matukio katika 12:1, na huenda yalijumuisha matukio yaliyo katika maono kutoka sura ya 11.

maneno yamefungwa na kutiwa chapa

Maono ambayo Danieli alikuwa amepewa hayakupaswa kufafanuliwa kana kwamba kitabu kilikuwa kimefungwa na hakuna mtu yeyote awezaye kukifungua.

wakati wa mwisho.

"siku za mwisho: au "mwisho wa ulimwenguni"

Daniel 12:10

Maelezo ya jumla

Malaika anaendelea kuongea na Danieli.

Watu wengi watakuwa wametakaswa, wameoshwa, na kusafishwa

Yahweh anafanya kazi ya kutakasa. Maneno haya matatu kimsingi yanamaanisha kitu kile kile.

kusafishwa

kusafishwa kwa kuondoa kila kitu kisichotakiwa sehemu ile.

lakini waovu wataenenda katika uovu

Watu waovu watateda yaliyo maovu au mambo ya dhambi.

Hakuna kati ya waovu atakayefahamu

Watu waovu hawawezi kufahamu mambo ya kiroho.

Lakini wenye hekima watafahamu

Hii inarejelea watu wale wenye hekima katika kumtii Yahweh watafahamu.

sadaka ya kawaida ya kuteketezwa ...imeondolewa

Mfalme wa Kaskazini ndiye atakayekomesha sadaka katika hekalu.

chukizo la uharibifu liliosababisha ukiwa

Hii inarejelea sana ambayo italifanya hekalu liwe ukiwa, na hiyo ndiyo itamsababisha Mungu aliache hekalu katika hali ya ukiwa.

siku zipatazo 1,290

Mahali hapa "siku" inarejelea kipindi cha muda. Mara nyingine hueleweka kama siku, ingawa pia ina maana ya miaka.

Daniel 12:12

Maelezo ya jumla

Malaika anaendelea kuongea na Danieli.

Ana heri mtu yule anayengojea

"amebarikiwa mtu ambaye anasubiri" au "ana heri yeyote anayengojea"

anayengojea

"kuvumilia" au "kubakia mwaminifu"

siku 1,335

Mahali hapa "siku" inarejelea kipindi cha muda. Mara nyingine hueleweka kama siku, ingawa pia ina maana ya miaka.

Unapaswa uondoke

"Danieli, lazima uende" Hii inamrejelea Danieli kuendelea kuishi na kumtumikia mfalme mpaka muda uliopangwa wa kifo chake.

utapumzika

Hii ni njia ya upole ya kusema kuwa "utakufa"

Utainuka

Hii inarejelea Ufufuo wa kwanza wa wafu wakati ambao watu wenye haki watafufuliwa.

ehemu uliyopewa

"sehemu ambayo Mungu amekupatia wewe"

Hosea 1

Hosea 1:1

Neno la Bwana lililofika

"Neno ambalo Bwana Mungu aslilisema"

Beeri.

Hili ni jina la mwanaume.

Uzia ... Yothamu ... Ahazi ... Hezekia ... Yeroboamu ... Yoashi

Matukio yaliyopo katika kitabu hiki yalitokea katika kipindi cha wafalme hawa.

Ukahaba mkubwa

"ukahaba" inawakilisha watu wanavyokuwa sio waaminifu kwa Mungu.

Hosea 1:3

Gomeri ... Diblaimu

Haya ni majina ya watu.

Nyumba ya Yehu

"nyumba" inamaanisha "familia" wakiwemo Yehu na uzao wake.

Nyumba ya Israeli

Maeliezo haya yanamaana ya ufalme wa Israeli.

Upinde wa Israeli.

Hapa "upinde" inamaana ya nguvu za jeshi. "nguvu za jeshi la Israeli"

Hosea 1:6

Lo Ruhama

Jina hili lina maana ya "sitawahurumia."

Hosea 1:8

Lo Ruhama

Jina hili lina maana ya "sitawahurumia."

Lo Ami

Jina hili lina maana ya "si watu wangu"

Hosea 1:10

Taarifa ya jumla

Bwana anazungumza na Hosea.

kama mchanga wa bahari

Hii inasisitiza idadi kubwa ya Waisraeli.

ambayo haiwezi kupimwa au kuhesabiwa

"ambayo hamna hata mmoja anayeweza kupima au kuhesabu"

Itakuwa pale ambapo waliambiwa

"Ambapo Mungu aliwaambia"

pale ambapo waliambiwa

Yamkini maneno haya yanaelekezwa kwa Yezreeli, mji ambao makosa yalifanywa na wafalme wa Israeli na ambayo ilikuwa ishara ya adhabu ya Mungu juu yao.

Wataambiwa

"Mungu atawaambia"

watakusanyika pamoja

"Mungu atawakusanya pamoja"

watatoka kutoka nchi

Hii inamaanisha nchi ambayo watu wa Israeli walichukuliwa mateka.

siku ya Yezreeli

Mungu atawaweka watu wake nyuma katika nchi ya Israeli.

Hosea 2

Hosea 2:1

Sentensi unganishi:

Bwana anazungumza na Hosea.

Watu wangu!

"Ninyi ni watu wangu"

umeoneshwa huruma.

"Bwana amewaonesha huruma"

Huruma

"wema" au "rehema"

Hosea 2:2

Taarifa ya jumla

Bwana anazungumza na Hosea.

Mashtaka

Haya ni malalamiko ya mtu mmoja dhidi ya mtu mwingine mahakamani.

Mama yako

Hapa "mama" inamaanisha taifa la Israeli.

kwa kuwa yeye si mke wangu

Bwana anaeleza kuwa Israeli inazungumzwa kama mwanamke ambaye hatendi kama mke kwa Bwana. Badala yake Israeli amegeuka na kuacha kumfuata na kumwabudu yeye.

wala mimi si mumewe

Bwana hawezi kuendelea kuwa na uhusiano na taifa la Israeli kama mume kwa mke wake.

na matendo yake ya uzinzi

Mke ambaye ni mzinzi anamuacha mume wake na kulala na mwanaume mwingine. Hivi ndivyo Israeli alivyofanya mbele ya Bwana.

kati ya matiti yake

Israeli wanategemea miungu na sio Bwana.

nitamvua nguo na kumuonyesha uchi wake kama siku aliyozaliwa

Bwana hataendelea kuwalinda na kuwasaidia Israeli kwa sababu taifa limemwacha.

nitamfanya kama jangwa

Bwana ataibadilisha Israeli ifanane na jangwa ambao nii mji usiozalisha.

nitamfanya afe kutokana na kiu

Hapa "kiu" inamaana ya uhitaji wa kumwabudu Bwana na sio miungu mingine, au Israeli hawatatweza kuishi kama taifa.

Hosea 2:4

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza na Hosea.

kwa maana wao ni watoto wa ukahaba.

Waisraeli wanafanya kama vile sio wa Bwana. Kama wazazi wao walivyofanya hawakumwabudu Mungu, na wao pia.

Maana mama yao amekuwa kahaba

Kizazi kilichopita waliitumikia miungu mingine na kuonekana kuwa ni makahaba kwa kuwa hawakuwa waaminifu kwa Mungu.

Nitawafuata wapenzi wangu, kwa maana wananipa mkate wangu na maji, sufu yangu na kitani, mafuta yangu na kinywaji.

Hapa "wapenzi wangu" inamaanisha Baali na miungu mingine ya uongo ambao Israeli walichagua kuiabudu badala ya Bwana.

Hosea 2:6

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza na Hosea.

Kwa hiyo nitajenga ua wa kuzuia njia yake kwa miiba. Nitajenga ukuta dhidi yake ili asiweze kupata njia

Maneno haya yanaonesha kuwa Bwana atawazuia watu wake wasipate mafanikio kwa sababu wanaiabudu miungu.

Kisha atasema, "Nitarejea kwa mume wangu wa kwanza, kwa maana ilikuwa ni bora kwangu zamani kuliko sasa."

Israeli watarejea kwa Bwana sio kwa sababu ya upendo wao kwake lakini kwa sababu wameumizwa kwa kumwabudu Baali.

Hosea 2:8

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza na Hosea.

Nitachukua sufu yangu na kitambaa kilichotumiwa kufunika uchi wake

Hii ina maana ya kwamba mavuno ya Israeli hayatakua. Bwana ataondoa baraka toka Israeli na watu wataachwa peke yao katika hatari.

kilichotumiwa kufunika uchi wake

"kitu ambacho watu hutumia kujifunika wenyewe"

Hosea 2:10

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza na Hosea.

nitamvua nguo machoni pa wapenzi wake

Hii inamaanisha Mungu atawaaibisha watu wa Israeli mbele ya mataifa mengine.

hakuna mtu atakayemwokoa mkononi mwangu

Hakuna mtu atakayewasaidia Israeli. Hapa "mkono" inamaana ya nguvu ya Mungu kuhukumu.

Hosea 2:12

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza na Hosea juu ya kile atakachokifanya kwa Israeli.

Hii ni mishahara ambayo wapenzi wangu walinipa

"huu ndio mshahara ambao atapewa na wapenzi wake"

Nitawafanya kuwa msitu

Bwana ataangamiza mizabibu na miti yake ya matunda kwa kuruhusu miti mingine na magugu kukua pamoja.

tamko la Bwana

"ambalo Bwana anasema"

Hosea 2:14

Sentensi unganishi:

Bwana anazungumza kuhusu Israeli.

hiyo nitaenda kumshawishi

"Mimi, Bwana nitamrudisha kwangu"

bonde la Akori kama mlango wa tumaini

Bwana atawaongoza Israeli tukoka Misri, atawaongoza Israeli katika bonde la Akori ili wamtumaini tena Bwana.

Yeye atanijibu huko kama alivyofanya katika siku za ujana wake, kama katika siku ambazo alitoka katika nchi ya Misri

Bwana anatumaini kwamba taifa la Israeli litatubu na kuchagua kumwabudu yeye kama Mungu wao.

Atajibu

Baadhi ya matolea ya kisasa ya kiebrania maneno haya yana maana ya "Ataimba."

Hosea 2:16

Itakuwa katika siku hiyo

Hii inamaanisha siku ambayo Israeli walichagua kumwabudu Bwana pekee.

tamko la Bwana

"Kitu ambacho Bwana amezungumza"

Mungu wangu

Hii inamaanisha watu wa Israeli watampenda na kuwa waaminifu kwa Bwana kama vile mke kwa mume wake.

Baali wangu

"Baali" inamaanisha miungu ya uongo ambayo Wakaanani wanaabudu.

Kwa maana nitaondoa majina ya Baali kinywani mwake

Waisraeli hawatataja majina ya Baali na miungu mingine.

Hosea 2:18

Sentensi unganishi:

Bwana anazungumza na Hosea kuhusu namna atakavyowafanyia Israeli.

Siku hiyo

Hii inazungumzia kuhusu urejesho wa baadae kati ya Israeli na Bwana.

Nitafanya agano kwao

Agano la Bwana litajumuisha amani kwa wanyama.

Nitaondoa upinde, upanga, na vita katika nchi, nami nitakufanya ulale kwa usalama.

Bwana atawaweka adui wa Israeli mbali na wao, hakutakuwa na vita tena watu watakuwa salama.

ulale kwa usalama

Kuishi kwa usalama.

Hosea 2:19

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza na Hosea kuhusu namna atakavyowafanyia Israeli.

Nitakuwa mume wako milele

Bwana atakuwa kama mume na Israeli atakuwa kama mke wa Bwana.

Nitakuwa mume wako kwa uaminifu

Bwana atakuwa mwaminifu kwa agano lake kwa Israeli.

mume kwa uaminifu

"mume mwaminifu"

Nawe utanijua mimi, Bwana

Hapa "kuniju" inamaanisha kumtambua Bwana kama Mungu na kuwa mwaminifu kwake.

Hosea 2:21

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza na Hosea kuhusu namna atakavyowafanyia Israeli.

ndilo tamko la Bwana

"Kitu ambacho Bwana amezungumza"

Dunia itashughulikia nafaka, divai mpya na mafuta, na watajibu Yezreeli.

Nchi itazalisha nafaka na divai mpya na mafuta.

Yezreeli

Jina la bonde hili linasimama kwa watu wa Israeli.

Hosea 2:23

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza na Hosea kuhusu namna atakavyowafanyia Israeli.

Nitatampanda mwenyewe katika nchi

Mungu atawaweka watu wake salama katika nchi yao tena. "Atawajali watu wa Israeli kama vile mkulima anavyopanda mazao yake na kujali"

Lo Ruhama

Jina hili lina maana ya "hakuna huruma."

Lo Ami

Hii ina maana ya "sio watu wangu."

Ami Ata

Jina hili lina maana ya "wewe ni mtu wangu."

Hosea 3

Hosea 3:1

"Nenda tena, mpendeni mwanamke, aliyependwa na mumewe; lakini ni mzinzi.

Bwana anamwambia tena Hosea ampende mwanamke mzinzi.

Mpende kama mimi, Bwana, ninavyowapenda watu wa Israeli

Kwa kumpenda mwanamke mzinzi, Hosea ataonesha mfano wa upendo wa Bwana kwa Israeli.

wanaigeukia miungu mingine na kupenda mikate ya zabibu.

Watu walikula mikate ya zabibu kipindi cha sikukuu walipokuwa wakiabudu miungu yauongo.

vipande kumi na tano vya fedha na homeri na letheki ya shayiri

Hii ndo ilikuwa gharama ya kununua mtumwa.

vipande kumi na tano

"vipande 15"

homeri na letheki

"homeri na nusu ya homeri"

Hosea 3:4

Kwa maana wana wa Israeli wataishi kwa siku nyingi bila mfalme, mtu mkuu, dhabihu, nguzo ya mawe, efodi au sanamu za nyumbani.

Kama vile Hosea hakuishi na mke wake kwa sababu alikuwa mzinzi, Israeli wataishi bila mfalme na bila kumwabudu Mungu kwa sababu wamefanya uzinzi.

kumtafuta Bwana Mungu wao

"kimtafta" inamaanisha kumwomba Mungu kuwakubali wao.

Daudi mfalme wao

"Daudi" inawakilisha uzao wote wa Daudi. "uzao wa Daudi utakuwa mfalme wao"

Na katika siku za mwisho

Hapa "siku za mwisho" inamaanisha kipindi cha baadae.

watakuja wakitetemeka mbele za Bwana na wema wake.

Hapa "kutetemeka" inawakilisha hisia za utu. "Walirejea kwa Bwana wakijinyenyekesha wenyewe, kumtii yeye na kuomba baraka zake"

Hosea 4

Hosea 4:1

Taarifa ya jumla:

Sura hii inaanza kwa kuonesha malumbano ya Bwana dhidi ya Waisraeli wasio waaminifu.

Bwana ana mashtaka dhidi ya wenyeji wa nchi

Bwana anaeleza kuwa wana wa Israeli wamefanya dhambi dhidi yake na kuvunja agano lake hii inazungumzwa kama vile Bwana anawashitaki mahakamani.

Mashitaka

Haya ni malalamiko ya mtu mmoja dhidi ya mtu mwingine mahakamani.

Watu wamevunja mipaka yote

"mipaka" ni mwisho wa vitu ambavyo sheria inaruhusu. "Watu wamevunja sheria kwa namna zote"

damu inakuja baada ya damu

"damu" inasimama kama mauaji.

Hosea 4:3

Kwa hiyo nchi inakauka

Maelezo haya yanamaanisha ukame ambapo mvua haijanyesha kwa muda mrefu.

Anaangamia

kuwa dhaifu na kufa kwa sababu ya ugonjwa au kukosa chakula.

wanaondolewa

"wanakufa"

Hosea 4:4

Taarifa ya jumla:

Mungu anazungumza juu ya Israeli.

Mashitaka

Haya ni malalamiko ya mtu mmoja dhidi ya mtu mwingine mahakamani.

msiruhusu mtu yeyote ahukumu mtu mwingine

Mtu yeyote asimuhukumu mtu mwingine kwa lolote kwa sababu kila mtu ni mkosaji wa jambo fulani.

Ninyi makuhani mtajikwaa

"kujikwaa" inamaanisha kutomtii Mungu na kuacha kumtumaini.

nitamwangamiza mama yako

Hapa "mama" inamaanisha taifa la Israeli.

Hosea 4:6

Taarifa ya jumla:

Katika 4:6 Bwana anazungumza na kuhani kuhusu watu wa Israeli. Lakini katika 4:7 anazungumza kuhusu kuhani na sio kwao.

Watu wangu wanaharibiwa kwa sababu ya ukosefu wa maarifa

"Watu wangu wanaharibiwa kwa sababu yenu, makuhani hamjawafundisha vema kuhusu mimi ili wanitii mimi"

Maarifa

Hapa "maarifa" inamaanisha maarifa juu ya Mungu.

Walibadilisha heshima zao kwa aibu

Yawza kuwa na maana ya 1) "heshima" inawakilisha Bwana, na "aibu" inawkilisha miungu. 2) Baadhi ya maandiko yametafsiri "Nitabadili heshima yao kwa aibu." Hii inamaana kuwa Bwana atachukua vitu ambavyo makuhani wanaviheshimu na kusababisha waaibike.

Hosea 4:8

Taarifa ya jumla:

Bwana anaendelea kuzungumza kuhusu makuhani.

Wanajilisha dhambi ya watu wangu

Watu walipotenda dhambi walitoa sadaka ili Mungu awasamehe. Makuhani waliruhisiwa kula sadaka hizo.

wao ni wenye tamaa zaidi ya uovu wao

Makuhani walitaka watu waendelee kutenda dhambi ili watoe sadaka ambazo makuhani watazila.

Itakuwa sawa kwa watu kama kwa makuhani

"Watu pamoja na makuhani watapewa adhabu ile ile"

matendo yao.

"tabia zao"

Hosea 4:10

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza juu ya Israeli.

lakini hawataongezeka

"lakini hawatakuwa na watoto"

wamekwenda mbali

Watu wameacha kumwabudu na kumfuata Mungu.

Bwana

Mtafsiri yupo huru kubadilisha "Bwana" na kuweka "mimi" kwa sababu Bwana ndiye anayeongea maneno haya.

Hosea 4:11

Taarifa ya jumla"

Bwana anazungumza juu ya Israeli.

uasherati, divai, na divai mpya, ambayo imechukua uelewa wao

Watu wa Israeli wanafanya uzinzi nje ya ndoa na wanakunywa sana mvingo. Kwa kufanya hivi wamesahau amri za Bwana.

fimbo zao za kutembelea huwapa unabii

Waabudu sanamu hutumia fimbo za kutembelea ili kutabiri yajayo.

mawazo ya uasherati yamewadanganya

Kuabudu miungu na kulala na wanawake makahaba wa hekaluni inawzfanya watu wa Israeli watamani kuendelea kutenda dhambi dhidi ya Bwana.

yamewadanganya

"kuwashawishi watu kufanya dhambi"

Hosea 4:13

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza juu ya Israeli.

juu ya milima ... kwenye milima

Ilikuwa ni kawaida watu kuweka miungu kwenye maeneo hayo, mara nyingi huitwa "sehemu za juu" katika agano la kale.

makahaba

Hawa ni wanawake wanaofanya uzinzi na wanaume wanaoenda kuabudu miungu fulani.

Hivyo watu wasiofahamu wataangamizwa.

Bwana ataangamiza taifa la Israeli kwa sababu hawakuelewe wala kutii amri za Mungu.

Hosea 4:15

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza juu ya Yuda na Israeli.

Yuda asiwe na hatia

Mungu anajua ni kwa kiasi gani Israeli wamefanya dhambi na hataki Yuda afanye kitu hicho hicho.

Ninyi msiende Gilgali; msiende hadi Beth Aven

Watu wa Yuda wanaonywa wasiende kwenye mji wa Gilgali au Beth Aven kuabudu miungu katika maeneo hayo.

Beth Aven

Huu ulikuwa mji uliokuwa kaskazini mpakati mwa ufalme wa Israeli na kabila la Benyamini lililopo kusini mwa ufalme.

kama ndama mkaidi

Israeli anafananishwa na ndama ambaye hamsikilizi bwana wake.

Je! Bwana anaweza kuwaleta kwenye malisho kama kondoo mahali penye nafasi?

Bwana hawezi kuwalisha watu kama kondoo wakati watu ni waasi.

Hosea 4:17

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza juu ya Israeli.

Efraimu alijiunga na sanamu; mwache peke yake

Efraimu ni watu wa kaskazini mwa ufalme wa Israeli. Walichagua kuabudu miungu badala ya Bwana. Bwana anamuamuru Hosea asijaribu kuwarekebisha maana hawatasikia.

watawala wake hupenda sana aibu yao

Viongozi hawaoni aibu ya kile walichokifanya wanapoabudu miungu na kugeuka dhidi ya Bwana.

Upepo utamfunga kwa mabawa yake

Hapa "upepo" unawakilisha hukumu ya Mungu na hasira juu ya taifa la Israeli. Bwana ataruhusu maadui wawashinde watu wa Israeli na kuwachukua mateka.

Hosea 5

Hosea 5:1

Sentensi unganishi:

Bwana anazungumza kuhusu Israeli.

Mmekuwa mtego huko Mizpa na wavu uliosambazwa juu ya Tabori.

Mtego na wavu ni vifaa vinavotumika kukatatia mawindo. Misoa na Tabori yalikuwa maeneo ya kuabudia miungu katika nchi ya Israeli.

Waasi husimama sana katika mauaji

"waasi" ni wale wote waliomuasi Bwana na mauaji inaelezea namna ambavyo mauaji ya watu wasio na hatia yanafanyika ikiwemo kutoa kafara kwa miungu ya kipagani.

Waasi

Mtafsiri anaweza kuiweka hii kama "ninyi waasi" kwa sababu Mungu anazungumza juu ya watu waasi wa Israeli.

mauaji

Baadhi ya nakala za kisasa za kiebrania neno hili limesimama kama uovu.

nitawaadhibu wote

"Nitawaadhibu ninyi nyote"

Hosea 5:3

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza kuhusu Israeli.

Najua Efraimu, na Israeli hajajificha kwangu

"Efraimu" na "Israeli" ni watu ambao wanaishi kaskazini mwa ufalme wa Israeli. Hapa Mungu anasema kuwa anawafahamu wao ni akina nani na nini wanafanya.

Efraimu, sasa umekuwa kama kahaba

Efraimu amesimama kama kahaba kwa sababu watu sio waaminifu kwa Mungu kama vile kahaba sio mwaminifu kwa mwanaume mmoja.

maana mawazo ya uzinzi yako ndani yao

Hii inamaanisha kuwa wanatamani kutokuwa waaminifu kwa Mungu. Wanataka kuabudu miungu.

kumgeukia Mungu ... hawatamjua Bwana.

"kunigeukia mimi ... hawakunijua mimi" au "kunigeukia mimi ... hawakunijua mimi, Bwana."

na hawatamjua Bwana

Israeli hawakumtii tena Mungu kwa namna yoyote. Hawakumtambua Bwana kama Mungu wao.

Hosea 5:5

Taarifa ya jumla:

Mungu anazungumza juu ya Israeli.

Kiburi cha Israeli kinawashuhudia

Hii inamaanisha kwamba tabia yao ya kiburi inaonesha kwamba wana makosa ya kutomtii Bwana.

hiyo Israeli na Efraimu watajikwaa kwa hatia zao; na Yuda pia wataanguka pamoja nao

Falme mbili zitaacha kumtii Mungu kabisa kwa sababu ya kiburi chao na dhambi yao.

Walikuwa wasio waaminifu kwa Bwana, kwa kuwa wamezaa watoto haramu

Hii yaweza kuwa na maana 1) Waisraeli walioa watu toka mataifa mengine na kuzaa watoto pamoja nao au 2) Wazazi wa Israeli hawakuwa waaminifu na waliwafundisha watoto wao kuabudu miungu.

Sasa sherehe mpya za mwezi zitawaangamiza na mashamba yao.

Wana wa Israeli walipaswa kusherehekea kipindi cha mwezi moya. Maelezo haya yanaonesha kuwa mwezi mpya ni mnyama atakayewala watu na mazao yao. maana ya jumla ni kwamba Mungu atawaadhibu watu kwa kutokuwa waaminifu kwake.

Hosea 5:8

Taarifa ya jumla:

Mungu anazungumza juu ya Israeli.

Piga tarumbeta huko Gibea, na tarumbeta huko Rama.

Amri inatolewa kwa watu wa Gibea na Rama kusistiza kuwa adui anakuja.

Sauti ya kilio cha vita huko Beth Aveni 'Tutakufuata, Benyamini!'

Hili ni ombi kuwa askari wa Benyamini wawaongoze watu katika vita.

Beth Aveni

Huu ni mji uliokuwepo mpakani kati ya ufalme wa kaskazini mwa Israeli na kabila la Benyamini kusini mwa ufalme.

Miongoni mwa makabila ya Israeli nimetangaza habari itakayotokea.

"Nitafanya katika kabila la Israeli yale niliyosema"

Hosea 5:10

Taarifa ya jumla:

Mungu anazungumza juu ya Yuda na Israeli.

Viongozi wa Yuda ni kama wale wanaoondoa jiwe la mipaka

"kuondoa jiwe la mpaka" ni kuondoa alama ya nchi inatoonesha mpaka wa mali ya mtu ambayo ilikuwa ni kosa kwa sheria za Israeli.

nitamwaga ghadhabu yangu juu yao kama maji

Hasira ya Bwana dhidi ya Yuda ni kama maji mengi yenye uwezo wa kuangamiza. Kwenye maandiko hisia na tabia zimefananishwa na kimiminika.

Efraimu ameangamizwa; ameangamizwa kwa hukumu

"Nitawaangamiza watu wa Israeli"

kufuata sanamu

"Kufuata" inawakilisha kitendo cha kuabudu miungu.

miungu

Neno la Kiebrania limetafsiriwa hapa kama "miungu" na katika tafsiri za kisasa limetafsiriwa kwa namna nyingi.

Hosea 5:12

Taarifa ya jumla:

Mungu anazungumza juu ya Yuda na Israeli.

nitakuwa kama nondo kwa Efraimu, na kama uozo kwa nyumba ya Yuda

Bwana ataangamiza mataifa yote.

Nondo ... uozo

Maneno haya yanatafsiriwa kwa njia mbali mbali kwa sababu maana ya kiebrania ni pana sana na isiyo na uhakika.

Efraimu alipoona ugonjwa wake, Yuda akaona jeraha lake

Efraimu na Yuda wote walitambua kuwa wapo kwenye hatari.

Efraimu akaenda Ashuru; Yuda akatuma wajumbe kwa mfalme mkuu

Efraimu na Yuda walimuomba Ashuru msaada badala ya kumuomba Mungu awasaidie.

Lakini hakuweza

Hapa anazungumziwa mfalme wa Ashuru.

Hosea 5:14

Taarifa ya jumla:

Mungu anazungumza juu ya Yuda na Israeli.

Kwa hiyo nitakuwa kama simba kwa Efraimu

Bwana ataenda kuishambulia Efraimu kama simba.

kama mwana simba kwa nyumba ya Yuda

Bwana atawatendea Yuda vivyo hivyo.

Mimi, naam mimi

Bwana anasisitiza kuwa yeye ataleta hukumu kwa watu wake wote.

Nitararua

Kama simba anavyorarua mnyama anayemla hivyo Bwana atawararua watu waketoka kwenye nyumba na nchi yao.

Nitakwenda na kurudi mahali pangu

Bwana atawaacha waasi.

na kutafuta uso wangu

Kujaribu kwenda katika uwepo wa Mungu kwa njia ya kuabudu na kafara.

Hosea 6

Hosea 6:1

Sentensi unganishi:

Wana wa Israeli wanaonesha uhitaji wao wa kutubu.

ametuvunja ...ametujeruhi

Mungu amewaadhibu wana wa Israeli kwa sababu hawakumtii na waliabudu Miungu.

atatuponya ... atatufunga majeraha yetu

Israeli wanaamini kwamba Mungu atawahurumia wakitubu na atawakomboa kutoka kwenye matatizo yao.

Baada ya siku mbili atatufufua; siku ya tatu atatuinua

Hii inawakilisha mda mfupi sana. Israeli wanaamini Mungu atakuja haraka kuwaokoa toka kwa adui zao.

siku mbili ... siku ya tatu

"siku 2 ... siku ya 3"

Nasi tumjue Bwana

"Kumjua" sio tuu kujifunza tabia za Bwana na sheria lakini pia kuwa mwaminifu kwake.

Kuja kwake ni hakika kama asubuhi

Bwana atakuwa kuwasaidia watu wake kama vile hakika jua linavyochomoza asubuhi.

Hosea 6:4

Sentensi unganishi:

Bwana anazungumza.

nikufanyie nini?

Mungu anaelezea kwamba subira yake inakaribia mwisho na kilichobaki ni hukumu.

Kwa hiyo nimewavunja vipande vipande kwa manabii

Kwa kupitia manabii wake, Bwana anatangaza kuangamiza taifa lililoasi.

Maagizo yako ni kama nuru inayoangaza

Hapa nabii Hosea anazungumza na Mungu. Anaweza kuwa na maana ya Mungu kutoa amri ya mtu kufa kama adhabu ni kama mwanga unaopiga. Au inaweza kuwa na maana kuwa Amri za Mungu zinawaruhusu watu kuijua kweli kama mwanga unaofanya vitu vionekane.

Maagizo yako

"Amri za Bwana"

Hosea 6:6

Taarifa ya jumla:

Bwama anazungumza.

natamani uaminifu wala si dhabihu

"kwa kuwa natamani uaminifu zaidi ya dhabihu"

Kama Adamu

Yaweza kuwa na maana ya 1) kumwelezea Adamu kama mtu wa kwanza au 2) inayowakilisha watu walioishi mjini Israeli wanaoitwa Adamu au 3) anawakilisha watu kwa ujumla.

Hosea 6:8

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza.

Gileadi ni jiji ... wenye miguu ya damu

"miguu ya damu" inawakilisha watu waovu na vitendo vyao vya uuaji.

makuhani hujiunga pamoja kufanya mauaji kwa njia ya Shekemu

Hatufahamu maneno haya yanamaanihs nini Hivyo ni vyema kutafsiri sentensi hii kwa namna ambayo itaeleweka zaidi.

Hosea 6:10

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza.

Uzinzi wa Efraimu

"uzinzi" inamaana kuwa Efraimu anaiabudu miungu ya uongo.

Israeli ametiwa unajisi

Israeli hajakubaliwa na Mungu kwa sababu ya vitendo vyake.

Kwa maana wewe, Yuda, mavuno yameteuliwa

"Nimetenga mda wa mavuno kwako pia , Yuda"

Mavuno

"Mavuno" inawakilisha siku ya Mungu ya mwisho ya hukumu kwa Israeli na Yuda.

Urihi

mafanikio na usalama

Hosea 7

Hosea 7:1

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza.

Nataka kuiponya Israeli

Kuifanya Israeli imtii Mungu tena na kitendo cha kupokea baraka kinazungumzwa kama kitendo cha uponyaji.

kwa sababu wanafanya udanganyifu

Watu walikuwa wanauza na kununua bidhaa kwa udanganyifu.

kundi la wanyang'anyi

Hili ni kundi la watu wanaowavamia watu wengine bila sababu.

matendo yao huwazunguka

Haya matendo yao maovu yanafananishwa na watu wanaliotayari kuwashitaki kwa maovu yao.

yapo mbele ya uso wangu.

"Uso" huu ni uwepo wa Mungu.

Hosea 7:3

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza.

Wote ni wazinzi

Watu wamefanya uzinzi wa kiroho kwa kuabudu miungu na kutokuwa waaminifu kwa Bwana. Pia hawakuwa waaminifu kwa wake zao na waume zao kwa kulala na watu wengine.

kama tanuru iliyochomwa na mwokaji

"kama tanuru ambalo mwokaji analichoma"

Kukanda unga

Hii ni moja ya hatua katika utengenezaji wa mkate.

Siku ya mfalme wetu

Yamkini hii ni sikukuu inayofanywa na mfalme.

Alinyoosha mkono wake

Hii inamaana kuwa mfalme ataungana na maofisa ili kuwadhihaki watu wasiopaswa kudhihakiwa na hata Mungu mwenyewe.

Hosea 7:6

Taarifa ya jumla:

Maafisa wa mahakama wanaelezewa. Hasira zao ziliwachochea kumuua mfalme.

kwa mioyo kama tanuru

Hii inamaanisha kuwa watu hawa walikuwa na nia ovu ndani mwao kama moto uwakao kwenye tanuru.

Hasira zao hulala

"hulala" Hii inamaanisha kuwa kitu kinachoungua taratibu.

huwaka juu kama moto

Hii inaonesha kuwa kiwango cha hasira yao ni kama moto mkali.

Wote wamepata moto kama tanuru

Hii inafananisha hasira yao na moto utakao kwenye tanuru.

huwaangamiza wale wanaowatawala

Hii inaonesha kuwa maofisa wa mahakama waliwaua wafalme wao.

Hosea 7:8

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza.

Efraimu anajichanganya mwenyewe kati ya watu

Hii inaelezea namna ambavyo wafalme wa falme za kaskazini walifanya kwa bidii kujichanganya na mataifa mengine kwa ajili ya ulinzi dhidi ya uvamizi.

Efraimu ni mkate ambayo haujawahi kugeuzwa

Efraimu ni ufalme wa Kaskazini wa Israeli. Taifa dhaifu kama mkate ambao haujageuzwa na mwokaji ili uwe na nguvu.

Nywele za mvi hunyunyiza juu yake

"nywele za mvi" zinawakilisha umri mkubwa.

lakini hajui

Huu "umri mkubwa" inaonesha wazi kuwa ufalme wa kaskazini ulikuwa dhaifu siku hata siku lakini mataifa hayajui kuwa inazeeka.

Hosea 7:10

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza.

Kiburi cha Israeli kinawashuhudia

Hii inamaanisha kwamba tabia yao ya kiburi inaonesha kwamba wana makosa ya kutomtii Bwana.

wala hawakumtafuta

Israeli waliacha kumtafuta Bwana.

licha ya hayo yote

Hapa "hayo" inamaanisha kitendo cha Mungu kuwaruhusu wageni wawashinde na kuwafanya dhaifu.

Efraimu ni kama njiwa, baradhuli na asiye na busara

Njiwa wanadhaniwa kuwa ni ndege wajinga.

Misri ... Ashuru

Haya ni mataifa yenye nguvu ambayo Israeli wangeomba msaada.

Hosea 7:12

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza.

nitasambaza wavu wangu juu yao

Hii ni njia ya kukamata ndege. Bwana anaendelea kuwafananisha Waisraeli na ndege. wakienda Misri kwa ajili ya msaada Bwana atawaadhibu.

nitawaangusha kama ndege wa angani

Bwana anazungumza namna atakavyowaangamiza Israeli kama vile atakavyomkamata ndege kwenye wavu.

katika kusonga kwao pamoja

Maelezo haya yanaendelea kusisitiza mfano wa ndege.

Hosea 7:14

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza.

wanaomboleza kwenye vitanda vyao

Ilikuwa ni kawaida kwa wanaoabudu sanamu kula nyama za sherehe wakiwa wamelala kwenye vitanda.

nao wananiasi mimi

Hawamwabudu tena Bwana wamegeuka na kumwacha.

Ingawa niliwafundisha na kuimarisha mikono yao

Mungu aliwafundisha Waisraeli kumpenda na kumtii yeye kitendo hiki kinazungumzwa kama kitendo cha kuwafundisha watu wake vita.

Hosea 7:16

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza.

Wao ni kama upinde usiotumainika

Huu upinde hautumiki.

kwa sababu ya udhalimu wa vinywa vyao

Hapa "vinywa" ni maneno yaliyosemwa na maofisa. "Kwa sababu wamenitukana mimi" au "kwa sababu wamenilaani mimi"

Hii itakuwa ni aibu yao katika nchi ya Misri.

"Hii ndiyo sababu kwamba Misri itawacheka Waisraeli"

Hosea 8

Hosea 8:1

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza kuhusu ujio wa jeshi la Waashuru kuvamia ufalme wa kaskazini.

Tai anakuja juu ya nyumba ya Bwana

Tai mara nyingine ametumika kuwakilisha maadui wa Israeli.

wamevunja agano langu

Hapa "kuvunja" inamaanisha "kutotii"

tunakujua

Hii ina maana ya kwamba "sisi ni waaminifu kwako"

Hosea 8:4

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza.

ili wakatiliwe mbali

Hii inaweza kuandikwa "lakini matokeo yake yatakuwa kwamba nitawaharibu watu hao"

Kukatwa

Kuharibiwa

Ndama yako imekataliwa, Samaria

Inaweza kuwa na maana 1) Kuhani anazungumza au 2) Bwana anazungumza. "Mimi mwenyewe nitakataa ndama yako, Samaria."

Ndama wako

Mfalme Yeroboamu wa pili wa Israeli alitengeneza miungu miwili ya dhahabu inayofanana na ndama na kuiweka juu ili watu wa ufalme wake waziabudu.

Hasira yangu inawaka juu ya watu hawa

Hasira inazungumzwa kama moto.

Kwa muda gani watakuwa na hatia?

Bwana anauliza swali ili kuonesha hasira yake kuhusu watu wake walio chafuka. "Nina hasira na watu hawa kwa sababu hawatamani kuwa salama"

Hosea 8:6

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza.

Kwa maana watu hupanda upepo na kuvuna kimbunga

Kupanda upepo ni kitendo cha kufanya jambo kwa njia zisizofaa. Kuvuna kimbunga ni kuteseka kutokana na matendo ya mtu mwenyewe.

Mbegu zilizosimama hazina vichwa

Hapa "kichwa" ni sehemu ya mmea mbayo mbegu zinakuwepo. Mmea ambao hauna kichwa unakuwa hauna chochote cha kumpa mkulima. Matendo ya Waisraeli hayatawapa matokeo mazuri.

Ikiwa itakomaa, wageni watakula.

Ikiwa matendo yoyote ya Waisraeli yatasababisha matokeo mazuri basi adui wa Israeli watayachukua.

Hosea 8:8

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza.

Israeli imemezwa

"imemezwa" inamaanisha imekamatwa na kupelekwa uhamishoni.

kama punda wa mwitu pekee

Hii inamaanisha kuwa wana wa Israeli walikataa kumsikiliza Bwana lakini badala yake wakaenda kwa Ashuru kuimba msaada.

Efraimu ameajiri wapenzi kwa ajili yake mwenyewe

Kitendo cha Efraimu kushirikiana na mataifa mengine kinazungumzwa kuwa ni kitendo cha kuwalipa kuwa makahaba kwa Efraimu. "Wana wa Israeli walijaribu kuwalipa mataifa mengine ili wawalinde"

kwa sababu ya unyanyasaji wa mfalme wa wakuu.

Kwa sababu mfalme wa Ashuru aliitwa "mfalme mkuu" atawafanya watu wateseke.

Hosea 8:11

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza.

Ningeandika sheria yangu kwao mara elfu kumi

Hii inamaanisha kwamba tayari Bwana aliwapa Israeli sheria yake kupitia manabii na kuwaambia ni kitu gani alitarajia kutoka kwao mara nyingi.

Elfu kumi

"10,000"

Hosea 8:13

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza.

Watarudi Misri

Kwa sababu ya uovu wao Mungu atarudisha watu wake wawe watumwa kwa Wamisri.

Hosea 9

Hosea 9:1

Taarifa ya jumla:

Nabii Hosea anazungumza.

Lakini sakafu na divai hazitawalisha

Hii inamaanisha kuwa mavuno hayatatoa nafaka ya kutosha kukidhi mahitaji ya watu na hakutakuwa na zabibu za kutosha kutengeneza mvinyo.

safafu ya kupuria

Hii ni sehemu kubwa inayotumika sio tuu kupuria nafaka lakini pia hutumiwa kwa sherehe za jamii na kidini.

divai mpya itampungukia.

Hakutakuwa na zabibu za kutosha kutengeneza mvinyo.

Hosea 9:3

Taarifa ya jumla:

Nabii Hosea anazungumza.

Nchi ya Bwana.

Hii inaonesha kuwa Bwana anaendelea kuiona nchi ya Israeli kama mali yake na sio mali ya Waisraeli.

Chakula kichafu.

Hiki ni chakula ambacho Waisraeli hawakula kwa sababu kiliwafanya wasikubalike kwa Bwana.

Dhabihu zao zitakuwa kwao kama chakula cha matanga

Hapa "chakula cha matanga" ni chakula kinacholiwa wakati watu wanaomboleza kwa sababu hawajakubaliwa na Mungu. Hii inamaana kuwa Bwana hataiona dhabihu yao kuwa ni chafu na hata wakubali.

Maana chakula chao kitakuwa chao pekee; hakitaingia nyumbani mwa Bwana.

Watu wa Israeli watakuwa na chakula lakini Bwana hataikubali kama dhabihu.

hakitaingia nyumbani mwa Bwana

Chakula kichafu kimezungumzwa kama kitu kinachoweza kwenda chenyewe. Watu huwa wanaenda nacho.

Hosea 9:5

Taarifa ya jumla

Nabii Hosea anazungumza.

Utafanya nini siku ya sikukuu iliyowekwa rasmi, siku ya sikukuu ya Yahweh?

Hosea anatumia swali hili kusisitiza kuwa watu hawataweza kushuhudia sikukuu zao ikiwa adui watawashinda na kuwashukua mateka.

siku ya sikukuu iliyowekwa rasmi ... siku ya sikukuu ya Yahweh

Zote hizi zina maana moja.

Kama wamekimbia

Hapa wanazungumziwa wana wa Israeli.

Misri itawakusanya, na Nofu itawazika

Misri na Nofu inamaanisha watu wanaoishi pale. "Jeshi la Wamisri litawakamata, mtakufa huko na watu wa mji wa Nofu watawazika"

Maana hazina zao za pesa- michongoma mikali itakuwa nao

Michongoma imeota sehemu ambayo Israeli walihifadhi fedha zao michongoma hii imefananishwa na adui ambaye atakuja kuchukua mali wanazomiliki Waisraeli.

michongoma itakuwa nao, na miiba itajaza hema zao.

"michongoma" na "miiba" inamaana moja. Michongoma na miiba ikiota inamanisha ardhi hiyo ni kama jangwa.

Hema zao

Hapa "hema" inawakilisha nyumba za Waisraeli.

Hosea 9:7

Taarifa ya julma:

Nabii Hosea anazungumza.

Siku za adhabu zinakuja; siku za kulipiza kisasi zinakuja

Hosea amesema kitu kile kile ili kusisitiza kuwa Bwana anakuja kuwahukumu watu wa Israeli kwa matendo yao maovu.

Nabii ni mpumbavu, na mtu aliyevuviwa ni mwendawazimu

Sentensi hii yaweza kuwa na maana 1) watu waliwaona manaabii kama wapumbavu au 2) manabii walichanganyikiwa kwa sababu ya dhambi zilizofanywa na watu.

Nabii ni mpumbavu, na mtu aliyevuviwa ni mwendawazimu

"nabii" na "mtu aliyevuviwa" zote zinamaanisha ni mtu anayesema kuwa amepokea ujumbe kutoka kwa Mungu.

kwa sababu ya uovu wako mkubwa na uadui mkubwa

"uovu mkubwa" na "uadui mkubwa" vina maana moja. Uovu wa watu unapelekea uadui dhidi ya Bwana na manabii wake.

Hosea 9:8

Taarifa ya jumla:

Nabii Hosea anazungumza.

Nabii ndiye mlinzi wa Mungu wangu juu ya Efraimu

"Mlinzi" hulinda nje ya mji wake kuangalia kama kuna hatari inakuja.

Nabii ndiye mlinzi wa Mungu wangu juu ya Efraimu

Nakala nyingine zimetafsiri sentensi hii kama "Nabii wa Mungu wangu ni mlinzi juu ya Efraimu.

Nabii ni

Hii inamaanisha manabii kwa ujumla ambao Mungu aliwachagua.

Efraimu

"Efraimu" inawakilisha watu wote wa Israeli.

mtego wa ndege ni juu ya njia zake zote

"mtego wa ndege" ni mtego unaotumika kukamata ndege. Hii inamaanisha kuwa watu wa Israeli walifanya kila wanaloliweza kumzuia nabii wa Mungu.

Wamejiharibu wenyewe kama siku za Gibea

"Wana wa Israeli wametenda dhambi na kujiharibu kama walivyofanya huko Gibea zamani"

Hosea 9:10

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza.

Nilipoikuta Israeli

Hii inaonesha mara ya kwanza Bwana alipoanza mahusiano na wana wa Israeli kwa kuwafanya watu wa pekee.

ilikuwa kama kutafuta zabibu jangwani. Kama matunda ya kwanza ya msimu kwenye mtini

Hii ina maana moja kusisitiza namna ambavyo Bwana alikuwa na furaha alipoanza mahusiano na watu wa Israeli.

Baal Peori

Hili ni jina la mlima katika nchi ya Moabu ambapo miungu ya uongo iliabudiwa.

Hosea 9:11

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza

utukufu wao utatoka kama ndege

Watu wa Efraimu watapoteza kila kitu kilichokuwa kinafanya mataifa mengine yawaheshimu. Utukufu wao utapotea haraka kama ndege apaavyo.

nikiwaacha

Mungu akiacha kuusaidia ufalme wa kaskazini itakuwa kama vile ameondoka kabisa kwao.

Hosea 9:13

Taarifa ya jumla:

Nabii Hosea anazungumza.

Nimeiona Efraimu, kama vile Tiro, alipandwa katika mlima

"kupandwa" ni kuwa sehemu salama. "Taifa la Israeli lilikuwa zuri kama mji wa Tiro, kama mti uliopandwa na mtu kwenye mlima"

akini Efraimu atatoa watoto wake

"watoto" ni watu toka kwenye taifa hilo.

Wape, Bwana-utawapa nini? Wape

Hosea ametumia swali kusisitiza kuwa anataka Bwana awape wana wa Israeli kile wanachostahili.

tumbo lenye kuharibu mimba

"kuharibu" inamaanisha ujauzito unakoma mapema na mtoto anakufa.

Hosea 9:15

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza.

nitawafukuza nje ya nyumba yangu

Bwana anasema kuwa atawafukuza Israeli kutoka kwenye nchi yake, nchi ya Kanaani.

Maofisa wao.

Watu wanaomtumikia mfalme.

Hosea 9:16

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza kwenye mstari wa 16. Hosea anaanza kuzungumza mstari wa 17.

Efraimu ni mgonjwa, na mizizi yao imekauka; hawazai matunda

Bwana anawazungumzia wana wa Israeli kama mti wenye ugonjwa usioweza kuzaa matunda na upo tayari kukatwa.

Hosea 10

Hosea 10:1

Taarifa ya jumla:

Hosea anazungumza juu ya Israeli.

Israeli ni mzabibu mzuri ambao huzaa matunda yake

Israeli inazungumzwa kama mzabibu unaozaa matunda.

Mzabibu mzuri

Mzabibu huu unatoa matunda kuliko kawaida.

kwa kadiri matunda yake yanavyoongezeka .... nchi uake inazalisha sana

Hii inamaanisha kuwa watu walinawiri na kuwe wenye nguvu na matajiri.

Moyo wao ni udanganyifu

"Wao ni wadanganyifu"

sasa wanapaswa kubeba hatia yao

"Sasa ni wakati ambao Bwana atawaadhibu"

Hosea 10:3

Taarifa ya jumla:

Hosea anazungumza juu ya Israeli.

Na mfalme-angeweza kutufanyia nini?

Watu watasema kuwa mfalme wao asingeweza kuwasaidia. "Hata tungekuwa na mfalme sasa asingeweza kutusaidia"

Wanasema maneno tupu

"maneno tupu" inamaanisha uongo. "Wanaongea uongo"

Kwa hivyo haki inakuja kama magugu yenye sumu katika mito ya shamba.

"Hivyo maamuzi yao sio ya haki, badala yake yana sumu"

kama magugu yenye sumu katika mito ya shamba

Uongo wao na kutotenda haki kunasambaa kwenye taifa na kuwadhuru watu kama mmea wenye sumu.

Hosea 10:5

Taarifa ya jumla:

Hosea anazungumza juu ya Israeli.

Beth Aveni

Huu ulikuwa mji uliokuwa kaskazini mpakati mwa ufalme wa Israeli na kabila la Benyamini lililopo kusini mwa ufalme.

watachukuliwa kwenda Ashuru

"Waashuru watawachukua"

Efraimu atakuwa na aibu, na Israeli atakuwa na aibu kwa sanamu yake

"Na watu wa Israeli wataaibika sana kwa sababu waliabudu miungu"

Sanamu yake

Nakala nyingi zimetafsiri neno hili la Kiebrania kama "mipango" au "mikakati"

Hosea 10:7

Mfalme wa Samaria ataangamizwa

"Waashuru watamwangamiza mfalme wa Samaria"

kama chipu cha kuni juu ya uso wa maji

Hii ina maana kuwa mfalme wa Samaria atakuwa hawezi kitu kama kipande kidpgo cha kuni kinachoelea juu ya maji"

Sehemu za juu za uovu zitaharibiwa

"Waashuru wataharibu sehemu za juu za Israeli ambazo watu walifanya uovu"

Watu wataiambia milima, "Tufunike sisi!" na kwa vilima, "Tuangukieni!"

"'watu watasema 'tunatamani milima itufunike!' na 'tunatamani vilima vituangukie!'"

Hosea 10:9

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza.

siku za Gibea

Hapa inaelezea matendo ya kushangaza ya kabila la Benyamini katika kitabu cha Waamuzi.

huko umebaki

Hii inamaanisha kuwa watu wa wakati huo waliendelea kufanya sawasawa na mababu zao walivyofanya huko Gibea.

Je, vita vitawapata wana wa uovu huko Gibea?

Bwana alitumia swali kusisitiza kuwa waliokuwa Gibea wakafanya uovu lazima vita vitawapata.

wana wa uovu

"wale wafanyao uovu"

Hosea 10:10

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza.

Uovu mara mbili

Hii inamaanisha uovu mwingi wa Israeli.

Efraimu ni ndama mwenye mafunzo ambayo anapenda kupura nafaka

Ndama anapenda kupura nafaka kwa sababu wanaweza kutembea kwa uhuru bila nira.

nitaweka nira juu ya shingo yake nzuri. Nitaweka nira kwa Efraimu

"Nira" inamaanisha mateso na utumwa. Bwana amekuwa mwema kwa wana wa Israeli lakini kwa sababu watu hawakuwa waaminifu atawaadhibu na kuwafanya watumwa.

Yuda ataimea; Yakobo atauvuta pigo kwa nafsi yake.

Bwana atasababisha wakati mgumu kwa falme zote za Yuda na Yakobo.

Pigo

Ni kifaa kinachotumika kuifanya ardhi iwe nzuri na kufunika mbegu baada ya kulima.

Hosea 10:12

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza.

ifanyieni haki, vuneni matunda ya uaminifu wa agano

Haki na agano vimezungumzwa kama mazao ambayo yanapandwa na kuvunwa.

Chimbueni ardhi yenu isiyopandwa

Ardi isiyolimwa haipo tayari kwa kupandwa. Bwana anataka watu watubu ili waanze kufanya mambo yanayofaa.

Mmelima uovu; mmevuna udhalimu.

Uovu na udhalimu vimezungumzwa kama mazao ambayo yanapandwa na kuvunwa.

Mmekula matunda ya udanganyifu

Matokeo ya udanganyifu yanazungumzwa kama chakula ambacho kinaweza kulika.

Hosea 10:14

Itakuwa kama Shalmani aliharibu Beth Arbeli siku ya vita

Vita inayokuja inafananishwa na vita ya zamani.

Shalmani

Hili ni jina la mfalme aliyeangamiza mji wa Beth Arberi miaka ya 740 kabla ya Kristo.

Beth Arberi

Hili ni jina la mji wa kabila la Naftali.

Kwa hiyo itakuwa kwako, Betheli, kwa sababu ya uovu wako mkubwa

Hapa "Betheli" inawakilisha watu wanaoishi pale. Nabii aliwaambia watu wa Betheli kama vile walikuwa wakimsikiliza.

Hosea 11

Hosea 11:1

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza namna anavyowajali Waisraeli kama mzazi anavyomjali mtoto.

Israeli alikuwa kijana

Bwana anazungumza juu ya wana wa Israeli kama watoto.

nikamwita mtoto wangu kutoka Misri

"mtoto" inamaanisha watu wa Mungu Baba. "Niliwaongoza watoto wangu kutoka Misri"

Kwa kadiri waliyoitwa, ndivyo walivyoondoka kwangu

"kwa kadiri nilivyowaita kuwa watu wangu ndivyo walivyokataa"

Hosea 11:3

Taarifa ya jumla:

Bwana anasema ni kwa namna gani anawajali Waisraeli.

Lakini mimi ndio niliyemfundisha Efraimu kutembea

Bwana anawaelezea Waisraeli kama watoto wadogo aliowafundisha kutembea.

niliyewainua kwa mikono zao

"kuwajali wao"

Niliwaongoza kwa kamba za ubinadamu, na mafungo ya upendo

Bwana aliwapenda watu wake kwa namna ambayo hakuna binadamu ambaye angeelewa na kujali.

Mimi nilikuwa kama mtu aliyepunguza jozi juu ya taya zao

Bwana anazungumza juu ya taifa la Israeli kama mnyama afanyaye kazi ngumu na kuifanya kazi yake kuwa rahisi.

nikainama na kuwalisha

Hii inamaanisha kuwa Bwana aliwapa mahitaji yao.

Hosea 11:5

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza juu ya Israeli.

Je, hawatarudi nchi ya Misri?

Swali hili linamaanisha kuwa taifa la Israeli watakuwa watumwa tena kama walivyokuwa Misri.

Je, Ashuru haitatawala juu yao kwa sababu wanakataa kurudi kwangu?

Taifa la Israeli litachukuliwa mateka na Ashuru kama matokeo ya kutokuwa waaminifu kwa Bwana.

Upanga utaanguka juu ya miji yao

Hapa "upanga" inawakilisha maadui wa Israeli watakao haribu miji ya Israeli.

kuharibu makomeo ya milango yao

Kuharibu makomeo inamaana ya kuondoa ulinzi wa watu.

ngawa wanaita kwa Aliye Juu

Hapa Mungu anajizungumzia mwenyewe. "Ingawa wataniita mimi, niliye juu"

hakuna mtu atawasaidia

Bwana hataruhusu mtu yeyote awasaidie Israeli kwa sababu wamemuacha.

Hosea 11:8

Taarifa ya jumla:

Bwana anaongea juu ya Israeli.

Ninawezaje kukuacha, Efraimu? Ninawezaje kukupeleka, Israeli?

Bwana anawapenda watu wake sana kiasi kwamba hatawaharibu kabisa.

Ninawezaje kukufanya kama Adma? Ninawezaje kukufanya kama Seboimu?

Bwana anawapenda watu wake sana kiasi kwamba hatawaharibu kabisa. "Sitaki kuwaangamiza kama nilivyoiangamiza Adma na Seboimu miji niliyoiangamiza pamoja na Sodoma"

Kwa maana mimi ni Mungu na wala si mtu

Mungu si kama mwanadamu anayeamua haraka kulipa kisasi.

Moyo wangu umebadilika ndani yangu

Hapa "moyo" unawakilisha mapenzi ya Mungu na maamuzi yake.

sitakuja katika ghadhabu

"Sitakuja kwako na kuwa na hasira na wewe"

Hosea 11:10

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza kuhusu lini atawakomboa watu wake.

Watanifuata, Bwana

Kumuabudu na kumuheshimu Bwana kunazungumzwa kama kitendo cha kumfuata nyuma yake.

Nitanguruma kama simba

Bwana atawafanya watu wake warudi kwenye nchi yake na kitendo hiki kimezungunzwa kama kitendo cha kuitwa.

Watakuja wakitetemeka kama ndege ... kama njiwa

Watarudi nyumbani mapema kama vile ndege anavyorudi kwenye kiota chake.

tamko la Bwana

"ambalo Bwana anasema"

Hosea 11:12

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza kuhusu Israeli na Yuda.

Efraimu ananizunguka kwa maneno ya uongo, na nyumba ya Israeli kwa udanganyifu

Vitendo vya uongo na udanganyifu vinazungumzwa ka vitu ambavyo watu wa ufalme wa kaskazini wamemzunguka navyo Bwana.

Lakini Yuda bado anaendelea nami

Watu wa ufalme wa kusini bado ni waaminifu kwa Mungu.

Hosea 12

Hosea 12:1

Taarifa ya jumla:

Nabii Hosea anazungumza.

Efraimu hujilisha upepo

Wana wa Israeli wanafanya mambo ambayo hayatawasaidia ni sawasawa na kujilisha upepo.

kufuata upepo wa mashariki.

Upepo wa mashariki ulikuwa na joto sana na wenye kuharibu. Hii inamaanisha kuwa majeshi kutoka mashariki ambayo Bwana atayatuma kuwaharibu wana wa Israeli.

huchukua mafuta ya Misri

Wana wa Israeli walipeleka mafuta kama zawadi kwa mfalme wa Israeli na kumsihi awasaidie.

Bwana pia ana mashtaka dhidi ya Yuda

Bwana anasema kwamba watu wa Yuda wamemtenda dhambi na kuvunja agano lake.

dhidi ya Yuda ... ataadhibu Yakobo ... kwa yale aliyoyatenda ... atamlipa kwa matendo yake

"Yuda" na "Yakobo" wote wanawakilisha watu wa Yuda.

mashitaka

Haya ni malalamiko ya mtu mmoja dhidi ya mtu mwingine mahakamani.

Hosea 12:3

Taarifa ya jumla:

Nabii Hosea anazungumza juu ya Yakobo baba wa Israeli.

Katika tumbo Yakobo akamshika ndugu yake kisigino

Yakobo alitaka kuchukua nafasi ya ndugu yake ya uzaliwa wa kwanza.

Alishindana na malaika akashinda

Yakobo alishindana na malaika ili malaika ambariki.

Hosea 12:5

Taarifa ya jumla:

Nabii Hosea anazungumza.

ndilo jina lake

"tunaomba kwa jina lake" au "tunaabudu kwa jina lake"

Shika uaminifu na haki la agano

Hii inamaanisha kutii amri za Mungu na kufanya mabo kwa usahihi.

Hosea 12:7

Taarifa ya jumla:

Nabii Hosea anazungumza juu ya Israeli.

mizani ya uongo

Wafanyabiashara wanatumia mizani kupima uzito wa fedha au bidhaa wanayonunua ua kuuza.

wanapenda kudanganya

Wafanyabiashara wanawadanganya wateja wao kwa kuchukua pesa nyingi kuliko inavyotakiwa.

Kwa hakika mimi ni tajiri sana; Nimepata utajiri kwa nafsi yangu

Sentensi hizi zina maana sawa kuwa watu wa Efraimu wanajiona kuwa wamefanikiwa sana.

Nimepata utajiri

Kuwa tajiri kwa kufanya biashara kunazungumzwa kama kupata utajiri.

hawataona uovu wowote ndani yangu, chochote ambacho kitakuwa dhambi

Watu wa Efraimu wanajiona kuwa ni watu wasio na lawama.

Hosea 12:9

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza na watu wa Israeli.

Mimi ndimi Bwana, Mungu wako, tangu ulipotoka nchi ya Misri

Hii inaweza kuwa na maana ya 1) "Mimi ni Bwana Mungu wako niliyewatoa baba zako toka nchi ya Misri" au 2) "Nimekuwa Mingu wako tangu ulipokuwa katika nchi ya Misri" au 3) "Nimekuwa Mungu wako ulipokuwa katika nchi ya Misri"

Nitakufanya uishi tena katika hema

Hii inaweza kuwa na maana ya 1) Bwana anawatoa kwa nguvu wana wa Israeli toka kwenye nyumba zao na kuwafanya waishi kwenye hema au 2) Ni ahadi kuwa baada ya uhamishi watu wataishi katika hema tena na Bwana atawatunza kama alivyofanya Misri.

Kwa mkono wa manabii

Hapa "mkono" unawakilisha mtu anayechukua hatua. "kupitia manabii"

Hosea 12:11

Taarifa ya jumla:

Nabii Hosea anazungumza.

madhabahu zao zitakuwa kama miundo ya jiwe katika miamba ya mashamba

Madhabahu ambazo watu wataabudia zitaangushwa chini na kuwa vipande vya mawe.

Yakobo akakimbia mpaka nchi ya Aramu; Israeli alifanya kazi ili kupata mke

"Yakobo" na "Israeli" ni majina ya mtu mmoja.

Hosea 12:13

Taarifa ya jumla:

Nabii Hosea anazungumza.

kwa nabii

Ambaye ni Musa.

amemkasirisha

Hasira ambayo mtu ameisababisha kwa Bwana ni kubwa mno.

Basi Bwana wake ataachia damu yake

Hapa "damu" ni hatia iliyopo kwa mtu aliyemuua mwenzake. Mungu haitaisamehe dhambi hiyo.

naye atamrudishia aibu yake

"atamfanya ateseke kutokana na matendo yake maovu"

Hosea 13

Hosea 13:1

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza.

Efraimu alipozungumza

Hosea ametumia neno Efraimu kumaanisha ufalme mzima wa kaskazini, japokuwa lilikuwa jina la moja ya makabila kumi na mbili.

kulikuwa na tetemeko

"kulikuwa na tetemeko kati ya watu"

Alijikuza katika Israeli

"kujikuza" ni kujifanya wa muhimu.

lakini akawa na hatia kwa sababu ya ibada ya Baali, naye akafa

Watu wa Efraimu walipoanza kuabudu Baali wakawa dhaifu na adui zao wakawashinda.

Sasa wanafanya dhambi zaidi na zaidi.

Hawa ni watu wa kabila la Efraimu na taifa zima la Israeli.

Watu hawa watoao dhabihu na kumbusu ndama

Sehemu ya kuabudu sanamu ni kwa kuibusu sanamu ambayo ni sanamu ya ndama.

Hosea 13:3

Kwa hiyo watakuwa kama mawingu ya asubuhi ... kama umande ... kama makapi ... kama moshi utokao kwenye bomba.

Maelezo haya yanaonesha kuwa Israeli itapotea kama itaendelea kuabudu sanamu.

yanayotokana na upepo

"ambayo upepo unavuma"

Hosea 13:4

Taarifa ya jumla:

Bwana anawazungumzia watu wake kama kundi la kondoo linalotangatanga jangwani.

Nilikujua jangwani

Bwana anasema kuwa Waebrania ni watu wake wa pekee na anawajali.

Wakati ulipokuwa na malisho, ulishiba

Sura ya kondoo inaendelea kuelezewa.

moyo wako ukainuliwa

"moyo" unawakilisha utu wa ndani wa mtu.

ukainuliwa

Kuwa na kiburi inazungumzwa kama kujiinua.

Hosea 13:7

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza.

kama simba ... kama chui ... kama dubu ... kama vile mnyama wa mwitu

Hawa ni wanyama wa porini ambao huvamia na kuwaua wanyama wengine.

kama dubu aliyenyang'anywa watoto wake

"kama dubu ambaye atashambulia mnyama atakayechukua watoto wake"

kama simba

"kama simba atakavyowala"

Hosea 13:9

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza.

nani atakayekusaidia?

"hakutakuwa na mtu wa kukusaidia wewe"

Mfalme wako yuko wapi, ili akuokoe katika miji yako yote? Wako wapi wakuu, ambao kwao umeniambia hivi, 'Nipe mfalme na wakuu'?

Bwana anauliza swali hili ili kuwaambia Waisraeli kwamba watakapoasi juu yake hakuna mfalme wala kiongozi atakayekuja kuwasaidia.

Hosea 13:12

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza.

Uovu wa Efraimu umehifadhiwa; hatia yake imehifadhiwa.

Sentensi hizi zina maana moja.

imehifadhiwa

Uovu wa ufalme wa kaskazini unazungumzwa kama kitu kinachoweza kuhifadhiwa.

Atakuwa na uchungu wa kujifungua,

Hapa Bwana anazungumzia mateso ya wana wa Israeli kama uchungu wa kuzaa.

lakini ni mwana mjinga, kwa maana wakati wa kuzaliwa, hatatoka tumboni

Bwana anawaelezea wana wa Israeli kama watoto wanaozaliwa. Watu hawataki kutubu na kumtii Bwana.

Hosea 13:14

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza.

Je, nitawaokoa na mkono wa kaburi? Je, nitawaokoa na kifo?

Bwana anatumia swali hili kuwaambia Waisraeli kuwa hatawaokoa na kifo. Lazima atawaadhibu.

Ewe Mauti yako wapi mapigo yako? Ewe kaburi kuko wapi kuharibu kwako?

Bwana anatumia swali kuwaambia kuwa atawaangamiza mda sio mrefu.

Huruma itafichwa

Huruma imezungumzwa kama kitu.

Huruma itafichwa na macho yangu.

"Sina huruma kwao"

Hosea 13:15

Taarifa ya jumla"

Nabii Hosea anazungumza.

Ndugu zake

Neno hili linasimama kuelezea mataifa yanayozunguka ufalme wa kaskazini, hasa Yuda ufalme wa kusini.

upepo wa mashariki utakuja; upepo wa Bwana

Upepo wa mashariki ulikuwa na joto sana na wenye kuharibu. Hii inamaanisha kuwa majeshi kutoka mashariki ambayo Bwana atayatuma kuwaharibu wana wa Israeli.

Kijito cha maji cha Efraimu kitauka, na kisima chake hakitakuwa na maji

Hosea anaendelea kuelezea ni kwa namna gani Mungu atawaadhibu wana wa Israeli.

ghala lake

Hivi ni vitu anavyomiliki mtu.

Hosea 13:16

Taarifa ya jumla:

Nabii Hosea anazungumza.

Samaria itakuwa na hatia, kwa sababu ameasi dhidi ya Mungu wake

"Samaria" inamaanisha watu wa mji wa Samaria walio na hatia ya uasi dhidi ya Mungu.

Wataanguka

Watu watakufa.

kwa upanga

Vitani.

watoto wao wadogo watavunjwa, na wanawake wao wajawazito watararuriwa wazi

"adui watawavunja watoto wao wadogo vipande vipande na kuwararua wazi wazi wanawake waajawazito"

Hosea 14

Hosea 14:1

Taarifa ya jumla:

Nabii Hosea anazungumza.

kwa kuwa umeanguka kwa sababu ya uovu wako.

Kutenda dhambi kunazungumzwa kama kitendo cha kuanguka.

Chukueni maneno pamoja nanyi

"kirini dhambi zenu"

matunda ya midomo yetu.

Kituatakachosema mtu ndiyo matunda na midomo.

Hosea 14:3

Taarifa ya jumla:

Hosea anazungumza.

kazi ya mikono yetu

"mikono" hii inamaanisha watu wanatengeneza vitu. "kwa sanamu tunazotengeneza"

mtu asiye na baba

Hii inaonesha huruma kubwa ya Mungu kwa watu wake.

hupata huruma

Hapa kitendo cha Mungu kuonesha huruma kinazungumzwa kama ni kitu ambacho mtu amekipata.

Hosea 14:4

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza.

Nitawaponya kugeuka kwao

Kuwafanya watu wasigeuke toka kwa Mungu kunazungumwa kama kitendo cha kuponya.

kugeuka kwao

Watu kushindwa kumtii Mungu kunazungumzwa kama kitendo cha kugeuka toka kwake.

Nitakuwa kama umande kwa Israeli; atachanua kama maua

Bwana anazungumza akijifananisha na umande unaohitajika ili kuupa rutuba mmea na Israeli inafananishwa na ua litakalochanua.

kuchukua mizizi kama mwerezi nchini Lebanoni

Taswira ya Israeli kama mmea inaendelea lakini hapa inafananishwa na mierezi wa Lebanoni.

Matawi yake yataenea ... kama mierezi ya Lebanoni

Sehwmu hii inaendelea kuzungumzia kitu hicho hicho.

Hosea 14:7

Taarifa ya jumla:

Bwana anazungumza.

Watu wanaoishi katika kivuli chake watarejea

Watu wa Israeli tena wataishi kwa kulindwa na Mungu.

watafufuliwa kama nafaka na maua kama mizabibu

Mafanikio ya Israeli yanazungumzwa kwa lugha ya kilimo.

Utukufu wake utakuwa kama divai ya Lebanoni

Kama divai ya Lebanoni ilivyokuwa maarufu pia Israeli itakuwa maarufu.

nifanye nini tena na sanamu?

Sentensi hii inaonesha kuwa Mungu atawakataza Israeli kuabudu muingu.

kama mberoshi majani yake ni ya kijani daima

Mberoshi ni mti ambao majani yake ni ya kijani mwaka mzima. Hii inawakilisha baraka za Bwana juu ya Israeli.

kwangu huja matunda yako

"matunda" inawakilisha kitu kizuri kinachotoka kwa Bwana.

Hosea 14:9

Taarifa ya jumla:

Nabii Hosea anazungumza.

Nani mwenye busara ili aelewe mambo haya? Nani anaelewa mambo haya ili awatambue?

Nabii anatumia maswali haya kusema kuwa watu wenye busara wataelewa na kusikiliza kile atakachokisema.

Kwa kuwa njia za Bwana ni sawa, na wenye haki watatembea ndani yao

Amri za Bwana zinazungumzwa kama njia ya kupitia.

wataanguka

Kutomtii Bwana kunazungumzwa kama kutendo cha kuanguka ukiwa unatembea.

Joel 1

Joel 1:1

Taarifa za jumla

Mungu anaongea kupitia Yoeli kwa watu wa Israeli wakitumia mashairi.

neno la Bwana lililomjia

"neno ambalo Bwana Mungu alinena"

Pethueli

Babayake Joeli

Je! Hii imewahi kuwa kabla ya siku zenu au katika siku za baba zenu

AT "Hii haijawahi kutokea kabla ya yenu au baba zenu"

Joel 1:4

Yale yaliyosazwa na tunutu

vikundi vingi vya wadudu kama viwavi vinavyoruka pamoja na kula maeneo makubwa ya mazao ya chakula

Tunutu ..... Nzige .... Panzi ... Madumadu

Hizi ni, kwa mtiririko huo, nzige wakubwa ambao wanaweza kuruka, nzige wawezao kuruka kwa urahisi, nzige wenye mbawa pia mdogo wa kuruka, na nzige wachanga ambayo bado hawajawa na mabawa. Tumia majina ambayo yataeleweka kwa lugha yako.

Joel 1:5

Taarifa za jumla

Mungu anawaonya watu wa Israeli kuhusu jeshi la nzige linaloja.

enyi walevi, lieni! Omboleza, ninyi nyote mnywao divai

Ikiwa lugha yako ina neno moja tu la 'kulia' na 'kusubiri,' unaweza kuunganisha mistari 'ninyi wanaopenda divai wanapaswa kulia kwa huzuni'

taifa

kundi nzige ni kama jeshi la kuvamia.

Meno yake ... ana meno ... Amefanya ... Ameondoa

Nzige ni kama taifa ambalo ni kama mtu mmoja. Unaweza kutaja taifa kama 'hilo,' au kwa nzige kama 'wao,' au kwa wavamizi kama mtu mmoja (ULB).

Meno yake ni meno ya simba, neye ana meno ya simba.

Mstari miwili ina maana sawa. Marejeleo ya meno ya nzige kuwa mkali kama meno ya simba hutia nguvu uharibifu ambao huwaangamiza kabisa mazao yote ya ardhi.

Nchi ya Bwana......shamba la mizabibu....mtini wangu

Nchi ya Bwana, shamba la mizabibu, na mtini

kutisha

Wale ambao wanaona ardhi hushangaa au kutisha kwa sababu imeharibiwa kabisa.

Joel 1:8

Taarifa za jumla

Mungu anaendelea kuongea na watu wa Israeli.

nchi imekuwa dhaifu

Hapa nchi inazungumzwa kama kama mtu. Hata hivyo, matoleo mengine hutafsiri kifungu hiki kama mfano tofauti "Nchi huomboleza."

Joel 1:11

Taarifa za jumla

Mungu anaendelea kuongea na watu wa Israeli.

shayiri

aina ya nyasi, kama ngano, ambayo mbegu zake zinaweza kutumiwa kufanya mkate

waliotauka

kukauka na kufa

tini .... komamanga .... epo

aina tofauti za matunda

Joel 1:13

Taarifa za jumla

Mungu anaongea na makuhani katika Israeli

Panda magunia na omboleza, enyi makuhani! Mwalia, enyi watumishi wa madhabahu. Njoo, ulala usiku wote kwenye magunia, enyi watumishi wa Mungu wangu

Mungu anawaambia makuhani kujinyenyekeza wenyewe na kulia kwa huzuni. AT 'Wote makuhani huomboleza na kuomboleza na kujinyenyekeza kwa kutumia usiku wote katika magunia"

sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji

sadaka ya kawaida katika hekalu

nyumbani mwa Mungu wenu

hekalu huko Yerusalemu

Joel 1:15

Taarifa za jumla

Hivi ndivyo Mungu anavyowaambia makuhani kusema.

Je, chakula hakikukatiliwa mbali mbele ya macho yetu, na furaha na kicheko kutoka nyumbani mwa Mungu wetu?

AT 'Tumeona vifaa vyetu vya chakula vilivyotumiwa, na wamevunja furaha na furaha kutoka kwa nyumba ya Mungu wetu.'

mbele ya macho yetu

'kutoka kwetu.' Hii inahusu taifa lote la Israeli.

furaha na kicheko

Maneno haya mawili yanamaanisha kimsingi kitu kimoja. Pamoja wanasisitiza kuwa hakuna aina ya shughuli za furaha zinazofanyika hekaluni.

Magunia

uvimbe wa uchafu

Joel 1:18

Taarifa za jumla

Mungu anaendelea kuwaambia makuhani jinsi wanapaswa kuomba kwa Israeli.

Huria

kufanya sauti ya kina kwa sababu ya maumivu

moto umekula ..... moto umeteketeza

Maneno haya mawili yanayofanana yanafanya kazi pamoja ili kuonyesha kwamba nchi yote, ingawa kulimwa au la, iliharibiwa.

imekauka

mito midogo

Joel 2

Joel 2:1

Taarifaza jumla

Joel anaendeleza mashairi ambayo yalianza katika sura ya awali.

Piga tarumbeta .... sauti ya kengele

Yoeli anasisitiza umuhimu wa kuwaita Israeli pamoja katika maandalizi ya uharibifu unaokuja.

siku ya giza na weusi

Maneno 'giza' na 'giza' yanashiriki maana sawa na kusisitiza ukubwa wa giza. Maneno mawili yanataja wakati wa maafa au hukumu ya Mungu. AT 'siku ambayo imejaa giza' au 'siku ya hukumu ya kutisha.'

weusi

giza kabisa au kwa kiasi

siku ya mawingu na giza nene

Kifungu hiki kinamaanisha kitu kimoja kama, na kuimarisha wazo la maneno ya awali. Kama vile maneno, wote 'mawingu' na 'giza giza' wanamaanisha hukumu ya Mungu. AT 'siku kamili ya mawingu ya dhoruba kali.'

Kama asubuhi inayoenea kwenye milima, jeshi kubwa na la nguvu linakaribia

AT "Jeshi kubwa, jeshi linakuja juu ya milima katika nchi. Wao husambaa juu ya nchi kama nuru kutoka jua inayoinuka "

jeshi kubwa na la nguvu

Maneno "kubwa" na "nguvu" yanashiriki maana sawa na hapa na kusisitiza nguvu za jeshi. AT "kundi kubwa la nzige" (UDB) au 'jeshi kubwa la binadamu.'

Joel 2:3

Taarifa za jumla

Maelezo ya Yoeli ya jeshi linalokuja yanaendelea.

nchi ni kama bustani ya Edeni

Bustani ya Edeni ilikuwa mahali pazuri.

Nchi hiyo ni kama bustani ya Edeni mbele yake, lakini nyuma yake kuna jangwa lililoharibika

Hii inaonyesha tofauti na kuonyesha uharibifu wa moto unaozalisha.

Joel 2:4

Taarifa za jumla

Maelezo yanaendelea na sauti za jeshi la farasi.

Farasi

Mnyama mkubwa na wa haraka na miguu minne.

Muonekano wa jeshi ni kama farasi

Mkuu wa nzige anaonekana kama kichwa cha farasi mdogo na jeshi ni kali na haraka kama farasi.

wanakimbia kama wapanda farasi

Jeshi linakwenda haraka, kama watu wanaoendesha farasi.

ruka

farasi anaruka au huruka kwa kasi kama anakimbia haraka.

kelele kama ile ya magari..... kama kelele za muale wa moto.... kama jeshi la nguvu lililo tayari kwa vita

Hizi zinalinganishwa na kelele ya jeshi la nzige.

Joel 2:6

Taarifa za jumla

Joel anaendelea kuelezea jeshi la nzige la Yahweh.

Wanakimbia kama wapiganaji wenye nguvu..... wanapanda kuta kama askari

Jeshi la nzige limeelezewa kuwa linafanya kama askari halisi.

kuta

kuta karibu na miji

Joel 2:8

Taarifa za jumla

Maelezo ya jeshi la nzige la Bwana yanaendelea.

wao huvunja kwa njia ya ulinzi

Waliwashinda askari wa kulinda mji.

Joel 2:10

Nchi hutikisika mbele yao, mbingu hutetemeka, jua na mwezi ni giza, na nyota zinaacha kuangaza.

Kuna nzige nyingi ambazo dunia na anga hutetemeka, na vitu vyote vilivyo mbinguni havionekani.

Bwana huinua sauti yake

Bwana akaonyesha uwezo wa Mungu na amri juu ya jeshi. AT "Yahweh ina udhibiti"

kubwa na yakutisha sana

Katika maneno haya yote maelezo yana maana kimsingi jambo moja. AT "kutisha sana"

Nani anayeweza kuishi?

AT "Hakuna mtu atakuwa na nguvu ya kutosha kuishi hukumu ya Bwana."

Joel 2:12

Nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote

AT 'Ondoa mbali na dhambi zako na kujitolea kikamilifu kwangu'

Rarueni miyoyo yenu, si mavazi yenu

Kuvaa nguo za mtu ni kazi ya nje ya aibu au toba. 'Kuvuta moyo' ina maana ya kuwa na mtazamo wa toba pia.

kugeuka

simama

Joel 2:14

Labda angegeuka ... Mungu?

Labda Bwana atageuka kutoka ghadhabu yake ... Mungu.

Joel 2:15

vyumba vyao.

vyumba, kwa kawaida katika nyumba za wazazi, ambapo wanaharusi watangojea sherehe zao za harusi

Joel 2:17

urithi wako

watu wa Israeli, ambao ni watu maalum wa Mungu

Kwa nini wanapaswa kusema kati ya mataifa, "Yuko wapi Mungu wao?"

AT "Mataifa mengine haipaswi kusema Mungu wa Israeli amewaacha watu wake."

Joel 2:18

nchi yake

Taifa la Israeli

watu wake

watu wa Israeli

Tazama

"Jihadharini na nini nitakavyosema"

aibu

"hastahili kuheshimu"

Joel 2:20

Taarifa za jumla

Mungu anaendelea ahadi yake kwa Israeli.

kaskazini .... mashariki....... magharibi

Maelekezo haya yanatoka kwa mtazamo wa watu wanaoishi katika nchi ya Israeli.

Joel 2:21

Msiogope, nchi

"Msiogope, enyi watu wa nchi,"

ya jangwa yatakua

mimea mzuri kwa ajili ya chakula itaongezeka juu ya nchi

mvua ya vuli na mvua ya masika

mvua za kwanza za msimu wa mvua, mapema Desemba na mvua za mwisho mwezi wa Aprili na Mei

Joel 2:24

vyombo

vyombo vingi vya vinywaji

miaka ya mazao ambayo nzige warukao walikula

'mazao uliyotunza kwa miaka mingi na kwamba nzige uliokwisha kula'

nzige warukao.... Palale, nzige wakuteketeza na nzige kuharibu

Angalia jinsi ulivyotafasiri maneno haya katika 1: 4.

Joel 2:26

Taarifa za jumla

Bwana anaendelea kuahidi mambo mema kwa ajili ya watu wa Israeli.

Joel 2:28

Taarifa za jumla

Bwana anaendelea kuahidi mambo mema kwa ajili ya watu wa Israeli.

nitamimina Roho yangu

"Nitawapa kwa ukarimu njia ambayo mtu humimina maji"

miili yote

"watu wote"

Joel 2:30

Taarifa za jumla

Bwana anaendelea kusema mambo ambayo atafanya wakati ujao.

damu, moto na nguzo za moshi

"damu" inaashiria kifo cha watu. AT "kifo, moto na nguzo za moshi"

na mwezi kuwa damu

Hapa neno 'damu' linamaanisha rangi nyekundu. Unaweza kutoa kitenzi cha maneno haya. AT 'na mwezi utakuwa nyekundu kama damu'

kubwa na ya kutisha

Hapa neno "kubwa" linabadili neno "la kutisha." AT "siku ya kutisha sana."

Joel 2:32

juu ya Mlima Sayuni na Yerusalemu

Hizi hutaja mahali sawa. AT 'juu ya Mlima Sayuni huko Yerusalemu.'

kati ya wale waliokoka, wale ambao Bwana anawaita.

AT "wale ambao Yehova anawaita watakuwa waathirika"

waliosalia

watu wanaoishi kuto kupatwa na tukio la kutisha kama vita au maafa

Joel 3

Joel 3:1

Taarifa za jumla

Mungu anaendelea kusema juu ya matukio ya baadaye.

Tazama

Neno "Tazama" hapa linaongeza mkazo kwa ifuatavyo.

katika siku hizo na wakati huo

Maneno 'wakati huo' yanamaanisha kitu kimoja kama, na inaongeza maneno 'katika siku hizo.' AT 'katika siku hizo' au 'wakati huo.'

nitakaporudi mateka wa Yuda na Yerusalemu

AT "Wakati mimi kutuma wahamisho nyuma kwa Yuda na Yerusalemu"

watu wangu na warithi wangu Israeli

Maneno haya mawili yanasisitiza jinsi Bwana anavyoona Israeli kama watu wake wa thamani. AT "watu wa Israeli, ambao ni urithi wangu."

walinunua kijana kwa ajili ya kahaba, kuuza msichana kwa divai ili waweze kunywa.

Hizi ni mifano ya aina ya mambo waliyofanya na haonyeshi kile walichofanya kwa watoto wawili. AT "na kufanya vitu kama biashara ya kijana kwa ajili ya kahaba na kuuza msichana kwa divai, hivyo wangeweza kunywa"

Joel 3:4

Taarifa za jumla

Mungu anaongea na watu wa mataifa yaliyozunguka Israeli.

kwa nini unanikasilikia

Mungu hutumia swali hili kuwashawishi watu wa Tiro, Sidoni na Ufalme. AT "Huna haki ya kunikasikia"

Je! mutanirudishia malipo?

'Je, utajipiza kisasi?' Mungu anatumia swali hili kuwafanya watu kufikiri juu ya kile wanachokifanya. AT 'Unafikiri unaweza kulipiza kisasi juu yangu'

mara moja nitawarudishia malipo yenu juu ya vichwa vyenu wenyewe

Hapa neno "kichwa' linamaanisha mtu. Kisasi ambacho walitaka kuelekea Bwana, atawafanyia. AT "Nitawafanya uhukumiwe kwamba ulijaribu kuniweka"

nitawarudishia

kulipiza kisasi" au "kulipa"

Joel 3:7

nje ya mahali ulipowauza

Watu wa Israeli watatoka mahali ambapo walikuwa watumwa na kurudi katika nchi ya Israeli.

kurudisha malipo

AT "kurudi kile unachostahiki"

kwa mkono wa watu wa Yuda

AT "kwa uwezo wa watu wa Yuda' au 'na watu wa Yuda"

Sheba

watu wa Sabea, ambayo pia huitwa Sheba. Watu hawa waliishi kusini mwa Israeli.

Joel 3:9

Jitayarisheni wenyewe kwa ajili ya vita ..... waamsheni mashujaa

Maneno haya yote yanasema kujiandaa askari kwa vita.

waamsheni mashujaa

"fanyeni watu wenye nguvu"

Yafueni majembe yenu kuwa panga na visu vyenu vya kuchongea kuwa mikuki

Maneno haya mawili yanashiriki maana sawa. Wote wawili anawafundisha watu kurejea zana zao za kilimo katika silaha.

majembe

zana ambazo hutumiwa kuvunja udongo ili kupanda mimea

Visu vya kuchongea

visu ambavyo hutumiwa kukata matawi madogo

Joel 3:11

jikusanyeni pamoja

"kusanyikeni pamoja kwa vita."

Bwana, washushe mashujaa wako.

Katikati ya ujumbe huu kwa maadui wa Israeli, hukumu hii inaelezwa kwa Yahweh. Labda hii ilikuwa kufanya maadui wao hofu ya jeshi la Bwana.

Joel 3:12

Taarifa za jumla

Bwana anaendelea kuongea na mataifa.

Naam, mataifa yajihimize yenyewe ..... mataifa yote ya jirani

Maneno 'mataifa' na 'mataifa yanayozunguka' yanataja mataifa yale yanayozunguka Yuda. Bwana atawahukumu katika bonde la Yehoshafati kwa yale waliyoyatenda Yerusalemu.

Wekeni katiki mundu.... pipa la divai limejaa

Inawezekana maana ni kwamba 1) mashambulizi ya mataifa ya dhambi ni kama kuvuna nafaka na kupiga zabibu, au 2) uharaka wa kuhukumu mataifa ya dhambi ni kama haraka ya kukusanya mazao yaliyoiva na kusagwa zabibu.

Wekeni katiki mundu, kwa maana mavuno yameiva

Bwana anaongea juu ya mataifa kama kama shamba la mazao yaliyoiva kwa ajili ya kuvuna. AT 'Weka sungura, kwa kuwa mataifa ni kama mavuno ya kuiva'

Wekeni katiki mundu

"Piga ngome kukata nafaka"

mundu

kisu cha muda mrefu ambacho watu hutumia kukata nafaka

mavuno yameiva

"nafaka iko tayari kuvuna"

Njoo, muponde zabibu, kwa ajiri pipa la divai limejaa

Bwana anasema juu ya mataifa kama kwamba walikuwa kundi la zabibu katika viti la mvinyo, tayari kwa watu kuwaponda. AT 'Njooeni, mkawaangamize mataifa, kwa maana wao ni kama zabibu katika divai'

Vipuri vilivyofurika, kwa sababu uovu wao ni mkubwa sana.

Bwana anasema uovu wa mataifa kama kama juisi iliyoyotoka kutoka kwenye divai ya maji hadi kwenye vats zilizokusanya. Vats sio vya kutosha kuwa na kiasi cha uovu unaoingia ndani yao.

Joel 3:14

mshtuko, mshtuko

Mshtuko ni kelele unasababishwa na umati mkubwa. Hii inarudiwa kuonyesha kuwa itakuwa kelele sana kutoka kwa watu wote.

bonde la hukumu

Maneno haya yanarudiwa kuonyesha kwamba hukumu hakika kutokea.

Joel 3:16

Bwana atasunguruma kutoka Sayuni, na kuinua sauti yake kutoka Yerusalemu

Neno zote mbili zinamaanisha Yahweh atasema kwa sauti kubwa, wazi na yenye nguvu kutoka Yerusalemu. Ikiwa lugha yako ina neno moja la kupiga kelele hii inaweza kutumika kama maneno moja. AT "Yahweh atasema kutoka Yerusalemu"

Bwana ataunguruma

Maana iwezekanavyo ni 1) 'Bwana atanguruma kama simba' au 2) 'Yahweh atanguruma kama radi.'

Mbingu na nchi zitatikisika

Sauti ya Bwana ni yenye nguvu sana kwamba itawafanya mbingu na dunia kutetemeka.

Bwana atakuwa makao kwa ajili ya watu wake, na ngome kwa wana wa Israeli

Maneno haya yote yanamaanisha Yahweh atawalinda watu wake. Ngome ni makazi yenye nguvu ya kulinda watu wakati wa vita. AT 'Yahweh atakuwa ngome yenye nguvu kwa watu wake'

Joel 3:18

Taarifa za jumla

Mungu anaendelea kusema juu ya siku ya Bwana.

milima itatiririsha divai nzuri

"divai nzuri hupungua kutoka milimani." Hii ni kisingizio kuonyesha kwamba ardhi ni yenye rutuba sana. AT "Katika milima kutakuwa na mizabibu inayozalisha mvinyo mzuri"

Milima itatiririsha maziwa

"maziwa yatatoka kutoka milimani." AT "juu ya milima mifugo na mbuzi wako watatoa maziwa mengi"

miito yote ya Yuda itapita katikati ya maji

"maji yatapita kati ya miito yote ya Yuda"

maji ya bonde la Shitimu

"atatuma maji kwenye bonde la Acacia." "Shitimu" ni jina la mahali upande wa mashariki wa Mto Yordani. Ina maana "Miti ya Acacia."

Misri itakuwa ukiwa

AT "Misri itaharibiwa na watu watakuacha" au "Mataifa ya adui ataharibu Misri na watu wa Misri wataondoka nchi yao"

Edomu itakuwa jangwa tupu

"Edomu itakuwa jangwa na watu watakuacha "

kwa sababu ya vurugu iliyofanyika kwa watu wa Yuda

"kwa sababu ya mambo mabaya Misri na Edomu waliwafanyia watu wa Yuda"

kwa sababu walimwaga damu isiyo na hatia katika nchi yao.

"damu isiyo na hatia" inamaanisha watu wasio na hatia waliouawa. AT "kwa sababu Misri na Edomu waliwaua watu wasio na hatia katika nchi ya watu wa Yuda"

Joel 3:20

Taarifa za jumla

Bwana anaendelea kusema juu ya siku ya Bwana.

Yuda utakua mwenyeji milele

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT 'Watu watakaa Yuda milele'

Yerusalemu itakuwa kizazi hata kizazi

Katika: "Uzazi baada ya kizazi, watu watakaa Yerusalemu"

Nitawalipizia damu yao, ambayo sijajilipizia kisasi

AT "Nitawaadhibu maadui ambao waliwaua watu wa Israeli na bado hawakuadhibiwa"

Amos 1

Amos 1:1

Mambo ambayo...Amosi...aliyapokea katika ufunuo

Kila kitu ambacho Mungu amemfanya Amosi kuelewa kupitia ambacho Amosi amekiona au kusikia.

Yahwe atanguruma kutoka Sayuni; atainua sauti yake kutoka Yerusalemu

Hii mistari miwili inashirikiana maana moja. Yote inasisitiza kwamba Yahwe anapiga kelele kama ajiandaa kulihukumu taifa

Yahwe atanguruma

kama 1) simba au 2) radi

Yahwe

Hili ni jina la Yahwe ambalo alijifunua kwa watu wake katika kipindi cha Agano la Kale. Tazama ukurasa wa tafsri ya Neno kuhusu Yahwe kuhusiana na jinsi ya kutafsiri hii.

Amos 1:3

Kwa dhambi tatu...hata kwa nne

"Kwa dhambi nyingi...kwa dhambi nyingi sana" au "Kwa sababu...ana dhambi nyingi sana, anamefanya dhambi nyingi sana kuliko niwezavyo kuruhusu"

sitabadilisha adhabu

"Hakika nitawaadhibu wale watu"

Amos 1:5

kumkatilia mbali mtu

Hapa "katilia" inamaanisha aidha "kuharibu" au " kutoa."

yule mtu ashikaye fimbo ya kifalme katika Beth Edeni

Baadhi ya matoleo ya kisasa yanatfsiri hii kuwa mtu mmoja aishiye katika Biqati Aveni

mtu ambaye aishiye katika Biqati Aveni.

Baadhi ya matoleo ya kisasa yametafsiri hii kumaanisha, "Watu ambao waishio katika Biqati Aveni." Matoleo ambayo yana "mtu" kawaida yanatafsiri hii maana dhahiri kumaanisha mfalme.

Biqati Aven...Beth Edeni...Kiri

jina la miji.

Edeni

tofauti na Bustani ya Edeni

yule mtu ashikaye fimbo ya kifalme

mfalme au mkuu

Amos 1:6

Kwa dhambi tatu...hata nne, sintobadilisha adhabu

tazama jinsi ya kutafsiri haya maneno katika 1:3.

Amos 1:8

katilia mbali

Hapa "Katilia" inamaanisha aidha "kuharibu" au kutoa."

yule mtu aishiye katika Ashdodi

Baadhi ya matoleo ya kisasa yanatafsri hii kumaanisha, "watu waishio katika Ashdodi." Matoleo ambayo yana "mtu" mara zote hutafsiri hii dhahiri kumaanisha mfalme.

mtu ashikaye fimbo ya kifalme kutoka Ashkeloni

Baadhi ya matoleo ya kisasa yametafsiri hii kuwa mtu mmoja anayeishi Ashdodi.

Nitaugeuza mkono wangu dhidi ya Ekroni

au "nitapigana dhidi ya Ekroni"

Amos 1:9

Kwa dhambi tatu...hata kwa nne, sintobadili adhabu

Tazama jinsi ya kutafsiri haya maneno katika 1:3

agano lao la undugu

"makubaliano waliyoyafanya kuwatendea kama kaka"

Amos 1:11

Kwa dhambi tatu...hata kwa nne, sintobadilisha adhabu

Tazama jinsi ya kutafsiri haya maneno katika 1:3.

ghadhabu yake ikabaki milele

"ghadhabu yake imebaki hata leo"

Bozra

Tazama: tafsiri ya majina

Amos 1:13

Kwa dhambi tatu...hata kwa nne, sintobadilisha adhabu

Tazama jinsi ya kutafsri haya maneno katika 1:3.

Amos 1:14

pamoja na dhoruba katika siku ya kimbunga

"pamoja na mambo mengi mabaya yanayotokea yote kwa pamoja"

dhoruba...kimbunga

aina mbili za upepo mkali sana

kimbunga

dhoruba ambayo iendayo kuzunguka katika duara.

Amos 2

Amos 2:1

"Kwa dhambi tatu...hata kwa nne, sintobadilisha adhabu

Tazama jinsi ya kutafsiri haya maneno katika 1:3.

chokaa

majivu yaliyobaki wakati

Amos 2:2

Keriothi

Tazama: tafsiri ya majina

Moabu atakufa

"Watu wa Moabu watakufa"

Amos 2:4

Kwa dhambi tatu...hata kwa nne, sintobadilisha adhabu

Tazama jinsi ya kutafsiri haya maneno katika 1:3.

Uongo wao

Hili neno hapa ni kama linamaasha "miungu ya uongo" au "sanamu."

kupotea...kutembea

Kuabudu sanamu imezungumziwa kana kwamba watu walikuwa wakitembea nyuma ya hawa miungu wa uongo.

Amos 2:6

Kwa dhambi tatu...hata kwa nne, sintobadilisha adhabu

Tazama jinsi ya kutafsiri haya maneno katika 1:3.

Amos 2:7

hekalu

dhuru kwa sababu maalumu na kurudi tena na tena kuendele

wanasukuma kukandamiza

"walikataa kusikiliza wakati ukandamizaji usemapo wanawatenda vibaya"

Amos 2:9

ambaye urefu wake ulikuwa kama urefu wa mierezi; alikuwa na nguvu kama mialoni

"ambao walikuwa warefu kama miti mirefu uijuayo na imara kama mti imara zaidi uujuayo"

Amos 2:11

Yahwe asemavyo

Mungu amesema

Amos 2:13

Tazama

"Sikiliza" au "Kuwa makini kwa kile ninachotaka kukwambai."

Amos 2:15

Apindaye upinde

"apindaye upinde atakimbia"

mkimbiaji sana hatakimbia

"mkimbiaji wa kwanza atanyakuliwa"

mwendesha farasi hatajiokoa

"mwendesha farasi atakufa"

kimbia uchi

Maana ziezekanazo 1) "kimbia bila silaha zake" au 2) "kimbia bila nguo."

Yahwe asemavyo

Mungu ameagiza.

Amos 3

Amos 3:1

neno

"Neno" linarejea kwenye kitu ambacho mtu amesema. Njia tofauti tofauti za kutafsiri neno "neno" au "maneno" inajumuisha, "kufundisha" au "ujumbe" au "habari" au "kusema" au "kilichosemwa." Wakati inamrejelea Yesu kama "Neno," hili neno lingetafsiriwa kama "ujumbe" au "usemi."

Yahwe

Neno "Yahwe" linatokana na jina ambalo alilojifunua wakati alipozungumza na Musa kwenye kichaka kilichokuwa kikiungua. Neno "Yahwe" linatokana na neno linalomaanisha, "kuwa" au "kuishi."

Israeli, Waisraeli, taifa la Israeli

Neno "Israeli" ni jina la Mungu alilokuwa amempa Yakobo. Linamaana, "amepambana na Mungu."

familia

Neno "familia" linarejea kwenye kundi la watu ambao wanauhusiano wa ndugu na kawaida inamuhusisha baba, mama, na watoto. Mara chache inawahusisha ndugu kama vile babu na bibi, wajukuu, wajomba na shangazi. Neno "familia" pia limetumika kurejea kwa watu ambao wanauhusiano kiroho, kama vile watu ambao ni sehemu ya familia ya Mungu kwa sababu wanamwamini Yesu.

Misri, Wamisri

Misri ni nchi katika upande wa kaskazini mwa Afrika, kuelekea kusini mashariki mwa nchi ya Kanaani. Mmisri ni mtu anayetoka nchi ya Misri.

aliyechaguliwa, chagua, watu waliochaguliwa, Aliyechaguliwa, teule

Neno, "mteule" maana halisi "waliochaguliwa" au "watu waliochaguliwa" na inarejea kwa wale ambao Mungu amewateua au kuwachagua kuwa watu wake. "Aliyechaguliwa" au "Aliyechaguliwa na Mungu" ni jina linalomrejea Yesu, ambaye ni Masiha aliyechaguliwa.

adhibu, adhabu

Neno "adhibu" linamaanisha kumsababisha mtu kuteseka kwa matokea hasi kwa kufanya jambo lisilo sahihi. Neno "adhabu" linarejea kwa matokeo hasi ambayo yametolewa kama matokeo ya hiyo tabia mbaya.

dhambi, enye dhambi, mwenye dhambi, kufanya dhambi

Neno "dhambi" linarejea kwa matendo, mawazo, na maneno ambayo ni kinyume na mapenzi ya Mungu na sheria. Dhambia inaweza kurejewa kwa kutokufanya kitu ambacho Mungu anataka tufanye.

Amos 3:3

Maelezo ya Jumla:

Mungu atajibu haya maswali katika 3:7.

Amos 3:5

Maelezo ya Jumla:

Mungu atajibu haya maswali katika 3:7.

Amos 3:7

Hakika Bwna Yahwe hatafanya kitu vinginevyo amewafunulia...manabii

"Bwana Yahwe atajifunua kwanza...manabii kabla hafanya chochote"

Amos 3:9

Yahwe asemavyo

Usemi wa Mungu.

Amos 3:11

kulalia

kiti kikubwa laini kwa kulala juu yake

pamoja na pembe ya kulalia, au pembe ya kitanda

Hiki kifungu kati Ebrania ni kigumu kuelewa, na baadhi ya matoleo yametafsiri kwa utofauti. Tafsiri ya UDB, imepangwa kwa baadhi ya matoleo ya kisasa, inatumia tashbihi. Inatamaana kwamba Waisraeli pekee wachache wataokoka, kama mmiliki wa nyumba angeweza kuokoa sehemu chache ya samani wakati nyumba yake inashika moto.

Amos 3:13

asemavyo Bwana Yahwe

Bwana Mungu Yahwe anazungumza.

pembe za madhabahu

Hizi zinaonekana kama pembe za ng'ombe zikitoka kutoka ambapo pande zote kuja pamoja kwa juu na zilikuwa alama kuonyesha jinsi mungu alivyokuwa hodari.

Amos 3:15

nyumba ya baridi pamoja na nyumba ya hari

"nyumba zote"

pembe

meno na pembe za wanyama wakubwa

asemavyo Yahwe

Mungu anazungumza.

Amos 4

Amos 4:1

watakapowaondoa kwa ndoana, wa mwisho wenu na ndoana za kuvulia samaki

Hii mistari miwili kimsingi inamaanisha kitu kimoja na kusisitia kwamba adui atawanyakua watu kama watu wakatavyo samaki. "kuwashinda wote na kuwalazimisha kwanda nao pamoja" au "kuwaweka juu ya ndoana kama samaki na kukuchukua."

Amos 4:3

bomolewa kwenye kuta za mji

Sehemu ambazo adui alizivunja chini ukuta wamji kuingia

mtajitupa mbele ya Harmoni

"watakutupa nje kuelekea Harmoni" au "maadui zako watakulazimisha kuondoka mjini na kwenda Harmoni"

Harmoni

Hii inaweza kuwa sehemu ambayo hatuijui. Au unaweza kurejelewa mlima wa Hermoni, na baadhi ya matoleo ya kisasa yameitafsiri kwa njia hii.

hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo

Hiki kirai kimetumika kuonyesha kwamba mambo aliyoyaongelea Mungu hakika yatatokea. Bwana Mungu anasema.

Amos 4:4

Nendeni Betheli na uovu, hata Gilgali mkaongeza dhambi

"Kwa sababu mmekataa kutubu, sadaka mtoazo katika Betheli na Gilgali pekee huniongeza asira zaidi"

leteni dhabihu zenu...zaka zenu...toeni sadaka za shukrani...tangazeni sadaka za hiar; zitangazeni

Kama lugha yako inanjia ya kuonyesha kwamba watu walikataa kuelewa kwamba kufanya haya mambo itawafanya vibaya lakini hayasimama kuwafanya, unaweza kutaka kuitumia hapa.

zaka zenu kila baada ya siku tatu

Badala ya "kila baada ya siku tatu," baadhi ya matoleo yana "kila baada ya miaka mitatu." Hi ni kwa sababu Waisraeli walitakiwa kuleta zaka zao kwa Mungu mara moja kila baada ya miaka mitatu.

asemavyo Bwana Yahwe

Bwana Mungu anasema.

Amos 4:6

usafi wa meno

"njaa" au "masumbuko"

hamkurudi kwangu

"hamjaacha kutenda dhambi juu yangu"

asemavyo Yahwe

Mungu Yahwe anazungumza.

Amos 4:8

Nimewapiga kwa maradhi yanayosababisha kuvu

"Wakati mwingine nawapatia mvua kidogo na wakati mwingine mvua kubwa"

maradhi

ugonjwa ambao unakausha na kuua mimea

ukungu

ukuaji mbaya kwenye vitu ambavyo vibakivyo na unyevu kwa mda mrefu

hamkunirudia

"hamjaacha kutenda dhambi juu yangu"

asema Yahwe

Bwana Mungu anazungumza.

Amos 4:10

kuufanya uvundo wa kambi zenu na kuingiza kwenye pua zenu

"Hewa iliyojazwa kwa

uvundo

harufu mbaya sana, hasa ya watu waliokufa

Milikuwa kama kijinga kilichokuwa kikiteketea kwenye moto

"Nimewavuta haraka kutoka kwenye moto kama mlikuwa kijinga kilichokuwa kikiteketea" au "Niwaache muungue sehemu kabla sijawavuta kutoka kwenye moto."

hamkunirudia

"hamjaacha kutenda dhambi juu yangu"

asema Yahwe

Mungu amezungumza

Amos 4:12

Israeli, Waisraeli, taifa la Israeli

Neno "Israeli" ni jina ambalo Mungu alimpa yakobo. Linamaana, "ameshindana na Mungu."

Mungu

Katika Biblia, neno "Mungu" linarejea kwenye kuwa milele aliyeumba ulimwengu wote kutoka bila kitu. Mungu anaisha kama Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu. Jina la Mungu ni "Yahwe."

funuo, ufunuo

Neno "funuo" maana yake kusababisha jambo kujulikana. "ufunuo" ni kitu ambacho kilichukuwa kimefanywa kujulikana.

mahali pa juu

Neno "mahali pa juu" linarejea kwenye madhabahu na sehemu takatifu iliyokuwa ikitumika kwa ajili ya kuabudu sanamu. Yalikuwa yamejengwa kawaida juu ya aridhi, kama juu ya mlima au pembeni ya mlima.

Amos 5

Amos 5:1

Bikira wa Israeli ameanguka...ata...ana...mwinue

"watu wa Israeli kikatili...wata...wame...wainue"

Amos 5:3

Bwana Yahwe, Yahwe Mungu

Katika Agano la Kale, "Bwana Yahwe" mara kwa mara limetuika limerejea kwa Mungu wa kweli mmoja."

nyumba

Neno "nyumba" mara nyingi limetumika katika Biblia.

Israeli, Waisraeli, taifa la Israeli

Neno "Israeli" ni jina ambalo Mungu alipatia Yakobo. Lina maana, "amepigana na Mungu."

Amos 5:4

Nitafuteni

"Njoo kwangu kwa ajili ya msaada"

Betheli haitakuwa kitu

"Betheli ataharibiwa kabisa" "watu watakuja na kuiharibu Betheli kabisa"

Amos 5:6

atawaka kama moto

"atakuwa kama moto uwakao ghafla na kuharibu kila kitu"

kugeuza kutenda haki kuwa jambo chungu na kuiangusha haki chini

kuita mambo maovu mema na kutenda mambo kama yasiyo muhimu

geuzao haki kuwa jambo chungu

au "kugeuza haki" au "kufanya isiyo haki lakini kusema ni haki"

kuiangusha haki chini

au "tena haki kama ingawa ilikuwa sio muhimu kama uchafu"

Amos 5:8

Pleidezi na Orioni

makundi ya nyota

Amos 5:10

kanyaga chini

"uonevu mkubwa"

Amos 5:12

kuwageuza wahitaji kwenye lango la mji

"msiwaruhusu maskini kuleta kesi zao kwa mahakimu"

kila mtu mwenye busara atanyamaza kimya

Wale ambao hawataki haki watu waovu kuwaumiza hawataongea kwa sauti juu ya matendo maovu.

Amos 5:14

imarisheni haki katika lango la mji

au "ona haki imetendeka katika mahakama kwenye malango ya mji"

Amos 5:16

Kuomboleza

mda mrefu, sauti, kilio cha huzuni

Amos 5:18

Kwa nini mnairefusha siku ya Yahwe?

"Msiirefushe siku ya Yahwe!"

Itakuwa giza na sio nuru

"Mambo mabaya, sio mambo mazuri, yatatokea siku hiyo"

Je siku ya Yahwe itakuwa giza na sio nuru?

"Siku ya Yahwe itakuwa giza hakika na sio nuru!" au "Mambo mabaya, sio mambo mazuri, yatatokea hakika katika siku ya Yahwe!"

Amos 5:21

Nachukia, nadharau sikukuu zenu

Neno "dharau" ni neno zito kwa "chuki." Kwa pamoja maneno yote mawili yanasisitiza msisitizo wa chuki ya Yahwe kwa ajili ya sikukuu zao za kidini. "Nachukia sikukuu zenu sana."

Amos 5:23

kelele

sauti mbaya

Amos 5:25

Je! Mmeniletea sadaka...Israeli?

Uweekano 1) "sijawaamuru mniletee matoleo...Israeli!" au 2) "hamkuleta matoleo kwa ajili yangu!" 2) "hamkuniletea matoleo kwa ajili yangu...Israeli!"

Sikuthi...Kiuni

miungu ya kipagani

Kiuni

Au "Kiyuni"

Amos 5:27

kuhamisha, uhamisho

Neno "uhamisho" hurejea kwa watu kulazimishwa mahali fulani mbali kutoka nyumbani kwao.

Damaskasi

Damaskasi ni mji mkubwa wa nchi ya Siria. Bado upo katika sihemu hiyo hiyo kama ilivyokuwa katika nyakati za Biblia.

Yahwe

Neno "Yahwe" ni jina binafsi la Mungu ambalo alijifunua wakati alipoongea na Musa katika kicha kilichokuwa kikiteketea.

Yahwe wa majeshi, Mungu wa majeshi, jeshi

Maneno "Yahwe wa majeshi" na "Mungu wa majeshi" kidogo yanaonyesha kwamba mamlaka ya Mungu zaidi ya maelfu ya malaika wanaomtii.

Amos 6

Amos 6:1

starehe

kustarehe na sio kuhusiana kwamba Mungu atawahukumu

Je ni wabora kuliko falme zenu mbili?

"Si wabora kuliko falme zenu mbili."

je mpaka mkubwa kuliko mpaka wenu

"Mipaka yao ni midogo kuliko yenu." au "Zile nchi ambazo ni ndogo kuliko Yuda na Samaria."

Amos 6:3

fanya ufalme kuwa kinyume kusogea karibu

"tenda katika njika ambayo Mungu ataleta watu wakali sana kuwahukumu"

ufalme wa kinyume

"adui wa kinyume na utawala"

lala...pumzika

Israeli katika kipindi kile kawaida walikuwa wakila wakiwa wameketi juu ya nguo ya sakafu au kwenye kti rahisi.

vitanda vya pembe

"vitanda pamoja na pembe juu yao kuwafanya kuonekana vizuri" au "vitanda vya gharama kubwa"

pembe

meno na pembe za wanyama wakubwa

pumzika

"kulala kama watu ambao hawataki kufanya kazi"

kochi

viti laini vikubwa kutosha kulala juu

Amos 6:5

wanatunga juu vyombo

Maana ziwezekanazo: 1) wametunga nyimbo mpya na njia ya kucheza vyombe au 2) wametunga ala mpya.

bakuli

bakuli zilitumika katika huduma za hekalu, kubwa kuliko zile zilizotumika kwa mtu katika mlo

hawahuzuniki

"hajisikii huzuni na kutenda kama kupitia yule aliyependwa aliyekufa"

Amos 6:7

asema Bwana Yahwe

Mungu mwenyewe anatoa maagizo.

Nachukia boma zake

"Nawachukia watu wa Israeli kwa sababu wanaamini boma zao, sio mimi, kuwalinda wao"

boma

kuta zilizojengwa kuzunguka miji kuwalinda kutoka kwa washambuliaji

Amos 6:9

ndugu wa mtu huyo atakapokuja kuchukua miili yao-yule ambaye awachomaye baada ya kuleta maiti katika nyumba-kama akisema kwa mtu katika nyumba,..."Je...wewe?

Mana ya haya maneno hayako wazi. "Ndugu wa huyo mtu" ni yule atakaye "chukua miili yao" na kuichoma...maiti," na akaongea na yule aliyejificha katika nyumba baada ya watu wa familia kumi kufa.

choma

choma maiti

maiti

miili iliyokufa

Amos 6:11

Tazama

"Sikiliza" au "Kuwa makini kwa kile ninachotaka kuwaambia."

nyumba kubwa itapigwa kuwa vipande vipande, na nyumba ndogo kuwa na nyufa

Hivi virai viwili vinashirikiana maana moja. Tofauti kati ya "nyumba kubwa" na "nyumba ndogo" inamaanisha kwamba hii inarejea kwa nyumba zote. Maana ziwezekanazo: 1) Yahwe atawaamuru wengine kuiharibu kila nyumba au 2) Yahwe mwenyewe ataiharibu kila nyumba mwenyewe kirahisi kwa kutoa amri.

nyumba kubwa itapigwa kuwa vipande vipande

"adui ataiseta nyumba kubwa kuwa vipande vipande"

kuwa vipande vipande...kuwa vipande

Unaweza kutumia neno hilo hilo kwa virai hivi vyote.

ndogo kuwa vipande vipande

"nyumba ndogo itasetwa kuwa vipande vipande"

Amos 6:12

Maelezo ya Jumla:

Amosi anatumia maswali mawili yasiyokuwa na majibu kuvuta mawazo kuwakemea hao wafuatao.

Je farasi watakimbia juu ya mteremko wa miamba?

Inawezekana kwa farasi kukimbia juu ya mteremko wa mwamba bila kuumia. Amosi anatumia swali hili lisilokuwa na majibu kuwaonya kwa matendo yao.

Je mtu atalima huko na ng'ome?

Mmoja hatalima juu ya mwamba. Amosi anatumia hili swali lisilokuwa na majibu kuwakemea kwa matendo yao.

Bado mmegeuza haki kuwa sumu

"Lakini umetengeneza sheria"

na tunda la haki kuwa uchungu

"na huwaadhibu wale wafanyao yaliyo haki"

Lo Debari...Karnaimu

Hakuna anayejua hii miji ilikuwa wapi.

Amos 6:14

tazama

"sikiiza" au "kuwa makini kwa kile ninachotaka kukwambai."

asema Bwana Yahwe

Hapa Mungu ananukuliwa.

kutoka Lebo Hamathi hata kijito cha Araba

"kutoka mpaka wa kaskazini mwa mchi yako hata mpaka wa kusini"

kijito

mto mdogo ambao hububujika kipindi cha majira ya unyevu pekee

Amos 7

Amos 7:1

Tazama...tazama

Mwandishi anawaambia wasomaji kwamba anataka kusema jambo la kushangaza. Lugha yako yaweza kuwa na njia ya kufanya hivi.

Je! Yakobo ataokokaje?

"Yakobo hawezi kuokoka"

Amos 7:4

Tazama

Mwandishi anamwambia msomaji kwamba jambo la kushangaza linalotaka kutokea. Lugha yako inaweza kuwa na njia ya kufanya hivi.

Je! Yakobo ataishije?

"Yakobo hataokoka hakika!" au "Tafadhali mwambie Yakobo kwamba anahitaji kufanya hivyo aweze kuishi!"

Amos 7:7

uzi wa timazi

kamba nyembamba pamoja na uzito upande mmoja wa mwisho uliotumika kuhakikisha kuta kusimama wima na chini

Amos 7:9

Isaka...Israeli

watu wa ufalme wa kusini mwa Israeli

Amos 7:10

Kuhani

Maana ziwekanazo: 1) Amazia alikuwa kuhani pekee katika Betheli au 2) Amazia mkuu wa makuhani katika Betheli.

amosi amefanya njama dhidi yako katikati ya nyumba ya Israeli

"Amosi yuko hapa katika nchi ya Israeli, na anapanga kufanya mambo mabay kwako"

Nchi haiwezi kubeba maneno yote haya

"Watu wanaweza kumwamini na kisha kufanya mambo mabaya yatakayo haribu taifa"

Amos 7:12

hapo ule mkate na kutabiri

"ona kama unaweza kuwapata watu huko wa kukulipa kwa ajili ya kutabiri"

Amos 7:14

mchungaji wa mifugo

Hii hapa ni kama inamaanisha "yeye ambaye achungaye kondoo" tangu aitwe "mchungaji" katika 1:1.

Amos 7:16

nchi najisi

Huu usemi unasimama hapa kwa ajili ya yeyote ngeni, ambapo watu hawakubaliki kwa Mungu.

Amos 8

Amos 8:1

Tazama

"sikiliza" au "Vuta usikivu kwa kile ninachotaka kukwambia."

Yahwe mwenye amezungumza

asemavyo Bwana Yahwe

katika kila mahali

"katika mahali pangu"

Amos 8:4

ninyi mkanyagao... na kumuondoa

Amosi anazungumza na wale ambao "huuza" na "soko"

hekalu

dhuru kwa sababu maalumu na kurudi tena na tena kuendelea

Husema, "Wakati mwezi mpya utakapoisha, hivyo tunaweza kuuza mazao tena? Wakati siku ya Sabato itakapoisha, ili kwamba tuuze ngano?

"Mara zote wanauiza ni lini mwezi mpya utaisha ili wauze nafaka tena, na ni lini Sabato itaisha ili wauze ngano."

Tutafanya kipimo kidogo na kuongeza bei, tukidanganya kwa mizani za udanganyifu

Wafanyabiashara wangetumia vipimo vya uongo vinavyoonyesha kile kiasi cha nafaka walichokuwa wakitoa kilikuwa kikubwa kuliko ilivyokuwa halisi na ule uzito wa malipo ulikuwa chini kuliko ilivyokuwa halisi.

na masikini kwa jozi moja ya kubadhi

"na nunua jozi moja ya kubadhi kwa ajili ya mhitaji"

Amos 8:7

Yahwe ameapa kwa fahari ya Yakobo

"Yahwe ameapa yeye mwenyewe, kusema" au Yahwe, ambaye ni fahari ya Yakobo, ameapa"

mto wa Misri

jina jingine kwa ajili ya Mto naili

Amos 8:9

asemavyo Bwana Yahwe

Mungu mwenyewe ameagiza hivo

Amos 8:11

asemavyo Bwana Yahwe

Mungu mwenyewe ameagiza

watatangatanga...watkimbia

Baadhi watatembea polepole na kuanguka chini kirahis, kama mtu mwenye njaa, na wengine watakuwa hapa na huko upesi.

kutoka bahari hata bahari; watakimbia kutoka kaskazini kwenda magharibi kutafuta neno

"kutoka bahari hata bahari na kutoka kaskazini hata magharibi. Watakuwa wakikimbia kutafuta neno."

kutoka bahari hata bahari...kutoka kaskazini kwenda magharibi

Kwa ajili ya mtu aliyesimama Betheli, hii ingeweza kuwa mduara: Bahari mfu (kusini) hata Mediterania (magharibi) hata kasikazini hata magharibi.

Amos 8:13

zimia

kupoteza nguvu zao zote

Kama njia ya iendayo Bersheba ionekanavyo

Hii ni kama kumbukumbu kwenye barabara ambayo wanaohiji wangeichukua kwenda Bersheba kwa ajili ya kuabudu sanamu huko.

Amos 9

Amos 9:1

Vivunje vipande

Maana ziwezekanazo: 1) kuvunja vipande vya hekalu au 2) vunja ncha za nguzo.

Hata kama watachimba kwenye Sheoli, kuna mkono wangu utawachukua. Hata kama watapanda juu kwenda mbingunu, huko nitawaleta chini

"Haijalishi wanajaribu kwenda wapi, intakuwa huko kuwashikilia."

Amos 9:3

joka

mnyama mkali wa baharini asiyejulikana, sio nyoka katika bustani ya Edeni na sio nyoka wa kawaida

Nitaelekeza macho yangu juu yao

Kama lugha yako inamaneno ambayo yanamaanisha mzungumzaji anataka kufanyia wengine mazuri lakini pia inaweza kutumika wakati mzungumzaji anapotaka kufanya madhara, unaweza kuitumia hapa.

na sio kwa uzuri

maneno kuhakikisha usikivu huelewa "kwa kuumiza"

Amos 9:5

yeye ndiye avijengaye vyumba vyake mbinguni

Hizi ni kama hatua ambazo watu wa kale walitafakari kuongozwa kwenda sehemu ya Mungu mbinguni. Ingawa, baadhi ya matoleo ya kisasa yanategemea kusoma neno la Kiebrania tofauti kumaanisha "mahali" au "vyumba." Hapa "hatua zake" ni kama hutumika kama kirai kwa ajili ya mahali pa Mungu.

na kuimarisha kuba yake juu ya dunia

Baadhi ya matoleo yametafsiri "ameimarisha mhimili wake juu ya dunia," hiyo ni, miundo ambayo dunia hupumzika.

Amos 9:7

asema Yahwe

Mungu mwenyewe amezungumza

Amos 9:9

mtu apepetaye ngano kwenye ungo, hivyo basi hakuna hata chembe ya jiwe itakayoanguka kwenye aridhi

Hapa ni picha ya nafaka zinazoanguka kwenye ungo na mawe kutolewa nje. Baadhi ya matoleo yanaelewa "sio mawe madogo yatakayoanguka" kumaanisha nafaka nzuri hazitaangukia kwenye ungo pamoja na malghafi yasiyohitajika.

ungo

uso wenye matundu madogo unaoruhusu vitu kupita na kuweka vitu vikubwa visipite

Amos 9:11

hema...matawi...magofu

Baada ya Yahwe kuuharibu ufalme wa Israeli, itakuwa kama hema ambazo nguzo zake za miti zimevunjika, ule ukuta uliokuwa umeanguka chini katika sehemu hiyo hiyo, na ile nyumba iliyokuwa imeangushwa chini.

matawi

sehemu za ukuta ambazo zimeanguka

magofu

kile kinachosalia wakati jengo limeharibiwa

mabaki ya Edomu

vyovyote kile ambacho Israeli haijatakiwa katika mkoa au watu wa Edomu.

Amos 9:13

Tazama

Mwandishi anawaambia wasomaji kwamba anaenda kusema jambo jipya. Lugha yako inaweza kuwa na namna ya kufanya hivi.

Milima itadondosha divai tamu, na milima yote itabubujika pamoja na hiyo.

Hii mistari miwili kimsingi ni kitu kimoja na kusisitiza kwamba nchi itazalisha sana.

Amos 9:14

hawatang'olewa tena kutoka kwenye nchi

"hakuna mtu atakayeweza kuwang'oa tena kutoka kwenye nchi" "wataishi milele katika nchi kama mmea uwekavyo mizizi yake kwenye aridhi"

ng'oa

vuta mmea mizizi yake nje ya aridhi

Obadiah 1

Obadiah 1:1

Bwana

Hii ni jina la Mungu ambalo aliwafunulia watu wake katika Agano la Kale. Angalia tafsiriKurasa la ukurasa kuhusu Yahweh kuhusu jinsi ya kutafsiri hii.

mjumbe ametumwa

AT 'Mungu alikuwa amemtuma balozi'

Inukeni

"simameni" Ukurasa huu umetumika kuwaambia watu kujiandaa.

Tazama

AT:"tazama" au "sikia" au " jiandae kwa kile ninachotaka kuwaambia"

mutadharauliwa sana

"watu wa mataifa wata waumiza ninyi"

Obadiah 1:3

Taarifa za jumla

Maono ya Obadia juu ya Edomu yanaendelea

Kiburi cha moyo wako

Bwana hutumia sehemu ya mwili wa mtu unaohusishwa na hisia kwa kutaja watu wa Edomu wanahisi kiburi.

katika makaburi ya mwamba

"katika nyufa katika miamba"

katika nyumba yako ya juu

"ndani ya nyumba yako iliyojengwa mahali pa juu"

Ni nani atakayenishusha mimi chini?

Swali hili linaonyesha jinsi Waedomu walivyojivunia na kujisikia salama. AT 'Mimi ni salama kutoka kwa washambuliaji wote.'

Ingawa unasimama juu kama tai na ingawa kiota chako huwekwa kati ya nyota,

Maneno haya yote yanasema Edomu imejengwa juu sana kuliko iwezekanavyo, kusema kuwa ilijengwa mahali pa juu sana.

Nitakushusha chini kutoka huko

Kiburi unahusishwa na urefu na unyenyekevu unahusishwa na kuwa chini. Bwana anasema atauleta Edomu kusema atashusha. AT 'nitakuwezesha'

Obadiah 1:5

Taarifa za jumla

Bwana anaendelea kumpa Obadia ujumbe wake kwa Edomu

kama wanyang'anyi walikuja usiku

"au kama wanyang'anyi walikuja wakati wa usiku"

wezi

watu wanaiba vitu kwa kuwa na vurugu kwa watu wengine

jinsi ungekatilwa mbali

Bwana anaongeza maneno haya katikati ya hukumu nyingine kuonyesha kwamba adhabu ya Edomu ni ya kushangaza. AT, ah, umeharibiwa kabisa.

Wasingeweza kuiba vya kuwatosha?

"wangeweza kuiba vinavyowatosha wenyewe."

Jinsi Esau amekwisha kupigwa, na hazina zake zilizofichwa zimewekwa nje

"Hakika, adui wamemtafuta Esau; wameitafuta hazina yake iliyofichika."

tafutwa

kutafuta vitu ili kuiba

Obadiah 1:7

Taarifa za jumla

Bwana anaendelea kumpa Obadia ujumbe wake kwa Edomu

ushirika wako

Neno "yako" linamaanisha taifa la Edomu.

Neno 'yako' linamaanisha taifa la Edomu.

"atakutuma nje ya nchi yao." Watu wa Edomu watajaribu kukimbilia katika nchi ya washirika wao, lakini washirika wao hawataruhusu watu wa Edomu kukaa katika nchi yao.

Hakuna ufahamu ndani yake

Edomu hawezi kuelewa

Je, si siku hiyo, asema Bwana, "kuharibu ... mlima wa Esau?

"Siku hiyo, asema Bwana," hakika nitauharibu ... mlima wa Esau. "

Watu wako wenye nguvu wataogopa

"Wapiganaji wako wenye nguvu wataogopa"

ili kila mtu apate kukatwa kutoka mlima wa Esau kwa kuchinjwa

AT "ili kuwa hakuna watu tena katika milima ya Esau kwa sababu maadui waliwaua."

mlima wa Esau

Nchi nyingi za Esau zilikuwa milima, kwa hiyo hii ni njia moja ya kutaja ardhi ya Esau.

Obadiah 1:10

Taarifa za jumla

Bwana anaendelea kumpa Obadia ujumbe wake kwa Edomu

ndugu yako Yakobo

AT "jamaa zako ambao ni wazao wa Yakobo."

utafunikwa na aibu

"utakuwa na aibu kabisa"

zitakatwa milele

"haitakuwepo tena."

alisimama karibu

"alitazama na hakufanya chochote kusaidia"

wageni

watu kutoka mataifa mengine

mali yake

Neno 'wake' linamaanisha 'Yakobo,' ambayo ni njia nyingine ya kutaja watu wa Israeli.

kupiga kura kwa ajili ya Yerusalemu

Maneno haya yanamaanisha 'walipiga kura ili kuamua nani atakayepata vitu muhimu ambavyo walichukua kutoka Yerusalemu.'

ulikuwa kama mmoja wao

"ilikuwa ni kama wewe ulikuwa mmoja wa wageni hawa na wageni"

Obadiah 1:12

Taarifa za jumla

Bwana anaendelea kumpa Obadia ujumbe wake kwa Edomu

usifurahi juu ya

"usifurahi kwa sababu ya" au "usifurahi"

Ndugu yako

Hii ilikuwa njia ya kutaja watu wa Israeli kwa sababu Yakobo na Esau walikuwa ndugu.

siku

"Siku ya adhabu" au "wakati wa adhabu."

bahati mbaya

'maafa' au 'shida'

katika siku ya uharibifu wao

"katika siku ambayo maadui wao atawaharibu"

siku ya dhiki zao

"kwa sababu ya wakati wao wanateseka"

msiba ... maafa ... uharibifu

Hizi ni tafsiri zote tofauti za neno sawa. Watafsiri wanapaswa kutumia neno moja kutafsiri yote haya matatu.

juu ya mateso yao

"kwa sababu ya mambo mabaya yanayotokea"

usipotee utajiri wao

"usichukue utajiri wao" 'au" usiiba utajiri wao"

njiapanda

mahali ambapo barabara mbili zinakuja ^ ^

ili kukata wakimbizi wake

"kuua watu wa Israeli ambao wanajaribu kutoroka" au "kukamata wale waliokuwa wakijaribu kutoroka" (UDB)

usiwape juu ya waathirika wake

"usiwape wale ambao bado wana hai na kuwapa adui zao"

Obadiah 1:15

Taarifa za jumla

Bwana anaendelea kumpa Obadia ujumbe wake kwa Edomu

Kwa maana siku ya Bwana iko karibu na mataifa yote

'Hivi karibuni wakati utakuja ambapo Bwana atawaonyesha mataifa yote kuwa yeye ni Bwana.'

Kama ulivyofanya, utafanyiwa kwako

"Nitawafanyia mambo yale uliyowafanyia wengine."

matendo yako yatarudi juu ya kichwa chako

AT "utapata matatizo kwa mambo uliyoyafanya."

Kwa vile wewe

Neno "wewe" kwa watu wa Edomu.

kama mlevi

Manabii huelezea watu ambao Bwana aliadhibu kama kunywa adhabu kutoka kwa Bwana AT 'kama nilivyowaadhibu.'

Mlima wangu mtakatifu

Hii ilikuwa njia ya kutaja Yerusalemu.

Mataifa yote yatakunywa daima

AT "Nitawaadhibu mataifa yote bila kuacha." Bwana aliadhibu Yerusalemu, lakini aliacha kabla ya kuwaangamiza watu wote. Hata hivyo, atawaadhibu mataifa yote mpaka hawako tena.

Obadiah 1:17

Taarifa za jumla

Bwana anaendelea kutoa Obadia ujumbe wake

kuokoka

"kukimbia adhabu ya Bwana." Hawa ndio watu ambao bado wana uhai baada ya Bwana kuwaaadhibu.

na hiyo

Neno "hilo" linamaanisha "mlima Sayuni."

nyumba ya Yakobo ... Josephu ni moto

Bwana anafananisha nyumba za Yakobo na Yosefu kwa moto kwa sababu wao watamwangamiza Esau kama moto ambayo haraka na kuchoma kabisa majani.

majani

"'majani" au "mchanga." Vipande vya kavu vya mimea ambazo zimeachwa baada ya nafaka huvunwa.

na wao

Neno "wao" linamaanisha nyumba ya Yakobo na nyumba ya Yosefu

watawachoma

Neno "wao" linamaanisha wana wa Esau, ambao ni taifa la Edomu

Hakutakuwa na waathirika kwa nyumba ya Esau

"Hakuna mtu mmoja wa nyumba ya Esau ataokoka'"

Obadiah 1:19

Benjamini

"kabila ya Benyamini' au 'watu wa Benyamini"

Obadiah 1:20

Wahamiaji wa jeshi hili la watu wa Israeli

"Wale wa jeshi la watu wa Israeli ambao walikuwa uhamishoni"

Jeshi

Kundi kubwa la watu

Zarefati

Hili ni jina la mji wa Foinike huko pwani ya Mediterranean kati ya Tiro na Sidoni.

Sefaradi

Hii ndiyo jina la mahali ambako eneo halijulikani.

waokoaji

Hii inahusu viongozi mbalimbali wa kijeshi wa Israeli ambao Mungu atatumia kushinda taifa la Edomu

Jonah 1

Jonah 1:1

neno la Bwana lilikuja

Hii ni idiamu ambayo inamaanisha Yahweh alisema. "Yahweh alizungumza ujumbe wake" (Angalia: tini_idiamu)

neno la Bwana

Hapa "neno" linawakilisha ujumbe wa Bwana. AT "ujumbe wa Bwana"

Bwana

Hili ni jina la Mungu ambalo aliwafunulia watu wake katika Agano la Kale. Tazama tafsiri ya ukurasa kuhusu Bwana jinsi ya kutafsiri hii.

Amittai

Hili ni jina la baba yake Yona. (Angalia tafsiri za majina)

Simama na uende Minawi, mji mkuu

"Nenda kwenye mji muhimu wa Minawi"

Amka na uende

Haya ni maelezo ya kawaida ya kusafiri kwa maeneo ya mbali.

piga kelele dhidi yake

"kuwaonya watu" (UDB). Mungu anawakilisha watu wa mji huo.

uovu wao umeinuka mbele yangu

"Najua wanaendelea kutenda dhambi"

akaondoka kukimbia kutoka mbele ya Bwana

"alikimbia kutoka kwa Bwana." "ameamka" inaelezea Yona aliondoka ambako alikuwa.

na akaenda Taeshishi

"na akaenda Tarshishi." Tarshishi ilikuwa kinyume cha Minawi. Hii inaweza kufanywa wazi. AT "na wakaenda kinyume chake, kuelekea Tarshishi"

Akatelemka mpaka Yafa

"Yona akaenda Yafa"

Meli

"Meli" ni aina kubwa sana ya mashua ambayo inaweza kusafiri baharini na kubeba abiria wengi au mizigo mizito.

Kwa hiyo akalipa nauli

Yona akalipia safari

na akapanda Meli

"na akaingia kwenye Meli"

pamoja nao

Neno "yao" linamaanisha wengine ambao walikuwa wakisafiri kwenye meli.

mbali na uwepo wa Bwana

Yona alitumaini kwamba Bwana hakuwapo Tarshishi

Jonah 1:4

Karibuni ikaonekana

Inaweza kufanywa wazi ambao walidhani meli itavunjwa. AT "Watu walidhani"(Angalia tini_zilizowazi)

inaweza kuvunjwa

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "kuvunja"

baharini

watu ambao walifanya kazi kwenye Meli

Mungu wake mwenyewe

Hapa "Mungu" ina maana ya miungu ya uongo na sanamu ambazo watu wanaabudu.

Wakatupa mizigo iliyokuwa kwenye Meli

'Watu walitupa vitu vikali sana kwenye meli.' Hii ilifanyika ili meli isiweze kuzama..

ili kuifungua

Kuifanya Meli iweze kuwa nyepesi na kuweza kuelea vizuri, AT: "kusaidia meli kuelea vizuri"

Lakini Yona alikuwa ameshuka kwenye sehemu za ndani za meli

Yona alifanya hivyo kabla ya dhoruba kuanza.

chini kataika sehemu za ndani ya Meli

"ndani ya Meli"

alikuwa amelala huko usingizi uliopitiliza

"alikuwa amelala haraka usingizi" au "alikuwa amelala pale na amelala kupitiliza." Kwa sababu hii, dhoruba haikumuamsha.

Jonah 1:6

Basi nahoza akamwendea akamwambia

"Mtu aliyesimamia meli akamuenda Yona na kusema"

kwa nini unalala?

"Kwa nini unalala?' Alitumia swali hili la uongo ili kumwambia Yona. AT "Acha kulala!"

Amka

Hii inamaanisha kufanya shughuli fulani. Kwa Yona, Kapteni anamwambia aamke na kumwomba mungu wake kwa kifungu salama.

Muite Mungu wako?

'Swali kwa mungu wako! "Piga" ina maana ya kupata tahadhari ya mtu.

Labda mungu wako atatutambua na hatutapotea

Maelezo ya wazi ambayo mungu wa Yona anaweza kuwaokoa inaweza kuwa wazi. AT "Labda mungu wako atasikia na kutuokoa ili tusife"

Wote wakaambiana

"Wafanyabiashara wote walisema"

'Njoni, tupige kura, ili tujue ni nani ndiye sababu ya mabaya haya yanayotupata.

Tunapaswa kupiga kura ili kujua ambaye amesababisha shida hii.' Wanaume waliamini kwamba miungu ingeweza kudhibiti jinsi kura ilivyoanguka ili kuwaambia nini walitaka kujua. Hii ilikuwa aina ya uchawi.

ubaya huu

Hii inahusu dhoruba kali.

Kura ikamuangukia Yona

"kura hiyo ilionyesha kwamba Yona alikuwa mtu mwenye hatia"

Jonah 1:8

Kisha wakamwambia Yona

"Kisha wale watu waliokuwa wakifanya kazi katika meli wakamwambia Yona"

Tafadhali tuambie ni nani ndiye sababu ya mabaya haya yanayotupata

"Ni nani aliyesababisha jambo hili baya ambalo linatupata?"

kumhofia Bwana

Neno "hofu" linamaanisha Yona anamheshimu sana Mungu.

Ni nini hiki ambaco umekifanya?

Watu katika meli walitumia swali hili la kuvutia ili kuonyesha jinsi walipokuwa wakiwa na uchungu na Yona. AT "Umefanya jambo baya."

alikuwa akikimbia mbele za uwepo wa Bwana

Yona alikuwa akimkimbia Bwana. Yona alikuwa akitaka kumkimbia Bwana kama Bwana alikuwapo tu katika nchi ya Israeli.

kwa sababu alikuwa amewaambia

Nini aliwaambia inaweza kuelezwa wazi. AT "kwa sababu alikuwa amewaambia "ninajaribu kuondoka mbali na Bwana"

Jonah 1:11

walimwambia Yona

"watu waliokuwa katika meli wakamwambia Yona" au "wasafiri walimwambia Yona"

tukutendee wewe ili kwamba Bahari iweze kutulia

"kufanya nawe ili kufanya bahari kuwa tulivu" (UDB)

bahari ilikuwa imechafuka zaidi na zaidi.

Hii ndiyo sababu watu waliuliza Yona nini wanapaswa kufanya. Sababu pia inaweza kupatikana mwanzoni mwa mstari wa 11 katika UDB.

kwa maana najua kwamba ni kwa sababu yangu kwamba tufani hii kubwa iwapate

kwa sababu najua dhoruba hii kubwa ni kosa langu'

Hata hivyo, watu hao wavuta makasia kwa bidii ili kurudi nchi kavu

Watu hawakutaka kumtupa Yona ndani ya bahari, kwa hiyo wakapiga kasia kwa nguvu kama vile wanalima ndani ya maji ili kurudi kwenye nchi

bahari ikawa imechafuka zaidi na zaidi

"dhoruba ikawa mbaya zaidi, na mawimbi yakawa kubwa"

Jonah 1:14

Kwa hiyo

Ilikuwa ni matokeo ya dhoruba ya kuwa mbaya zaidi ambayo ilisababisha jibu la pili. AT "Kwa sababu bahari ikawa imechafuka zaidi"

akamlilia Bwana

watu wakamuomba bwana

usiache tuangamize kwa sababu ya maisha ya mtu huyu

"Tafadhali usituue kwa sababu tumemfanya mtu huyu afe' au 'Tutakwenda kusababisha mtu huyu afe. Lakini tafadhali usituue"

wala usituwekee hatia ya kifo chake

"na tafadhali usitulaumu kwa kifo chake" au "wala usichukue hatia wakati mtu huyu akifa." Mwandishi anazungumzia "hatia" kama ni kitu ambacho kinaweza kuwekwa juu ya mtu. Inahusu kumfanya mtu huyo awejibika kwa matendo yao.

bahari ikaacha kuchafuka

"bahari iliacha kusonga kwa ukali" au "bahari ikawa tulivu" (UDB

walimuogopa sana Bwana

"walishangaa sana kwa nguvu za Bwana" (UDB)

Jonah 1:17

Taarifa za jumla

Baadhi ya namba za matoleo kama mstari wa kwanza wa sura ya 2. Unaweza kutaka kuhesabu mistari kulingana na toleo kuu ambayo kikundi chako cha lugha hutumia.

Sasa

Neno hili linatumika kwa Kiingereza ili kuanzisha sehemu mpya ya hadithi.

siku tatu na usiku wa tatu

"siku tatu na usiku "

Jonah 2

Jonah 2:1

Bwana Mungu wake

Hii inamaanisha "Bwana", Mungu aliyemwabudu." Neno "wake" haimaanishi kwamba Yona alikuwa na Mungu.

Akasema

"Yona akasema"

Nimemwita Bwana juu ya shida yangu

'Nilimwomba Bwana kuhusu shida yangu kubwa.' Ingawa Yona alikuwa akimwomba Bwana, alitumia jina la Bwana hapa na si "wewe." AT "Bwana, nimekuita juu ya shida yangu'

naye akanijibu

"Bwana alinijibu" au "alinisaidia"

kutoka tumbo la Kuzimu

"kutoka katikati ya Kuzimu' au 'kutoka sehemu ya kina ya Kuzimu.' Inawezekana maana ni 1) Yona alikuwa akizungumza kama alikuwa ndani ya tumbo la nyangumi alikuwa akiwa Kuzimu au 2) Yona aliamini kwamba alikuwa karibu kufa na kwenda Kuzimu au 3) Alizungumza kama alikuwa amekufa na kwenda huko.

Jonah 2:3

Taarifa za jumla

Huu ni muendelea wa sala ya Yona ambayo ilianza katika 2 :1. Katika mstari wa 4 Yona alizungumza juu ya kitu ambacho alikuwa ameomba kabla ya sala hii.

katika kina, ndani ya moyo wa Bahari

Hii inazungumzia ukubwa wa bahari alipokuepo Yona

ndani ya moyo wa bahari

"chini ya bahari"

maji yaliyonizunguka

"maji ya bahari yalikuwa karibu kunizunguka"

mawimbi na gharika

Kulikuwa na mvurugo juu ya uso wa bahari. ((Angalia tini_ufunua))

Nimefukuzwa nje

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "Umenifukuza mbali" au "Umeniacha" (Angalia tini_washiriki)

kutoka mbele ya macho yako

"kutoka kwako." Yona aliposema "macho yako" alikuwa akisema juu ya Bwana kwa ukamilifu wake.

lakini nitaangalia tena juu ya hekalu lako takatifu

Yona ana matumaini kwamba, licha ya yote anayopita, ataona hekalu. (Angalia tani_kutaja)

Jonah 2:5

Taarifa za jumla

Huu ni muendelezo wa sala ya Yona iliyoanzia 2:1

Maji

"Maji" yanarejea kwenye bahari

shingo yangu

Matoleo mengine huelewa neno la Kiebrania katika neno hili kwa maana ya "maisha yangu." Katika tafsiri hiyo, maji yalikuwa karibu kumchukua maisha ya Yona.

kina kilinizunguka

"maji ya kina yalikuwa yakinizunguka"

mwani

"nyasi zinazopandwa baharini"

nchi na baa zake zimefungwa juu yangu milele

Yona alitumia mfano wa kulinganisha dunia na gerezani. Kwenye "dunia ilikuwa kama gerezani ambayo ilikuwa karibu kunifunga kwa milele" (Angalia tini_mapira)

Lakini wewe umeinua uhai wangu shimoni

Yona anazungumzia mahali pa wafu kama kama shimo. AT "Lakini umeokoa maisha yangu kutoka mahali pa wafu" au "Lakini umeniokoa kutoka mahali ambako watu wafu' "(Angalia tini_mapira)

Bwana, Mungu wangu!

Katika lugha zingine, inaweza kuwa ya asili zaidi kuweka hii mwanzo wa sentensi au karibu na neno "wewe."

Jonah 2:7

Taarifa za jumla

huu ni muendelezo wa sala ya Yona iliyoanzia 2:1

nikamuita Bwana

Tangu Yona alipomwomba Bwana, inaweza kuwa wazi zaidi katika lugha zingine kusema "Nilifikiri juu yako, Bwana" au "Bwana", nilifikiri juu yako." (UDB)

basi sala yangu ilikujia, katika hekalu lako takatifu

Yona anasema kama sala zake zinaweza kusafiri kwa Mungu na hekalu lake. AT "basi wewe katika hekalu lako takatifu liliisikia sala yangu" (Angalia tini_mapira)

Wale wanaozingatia miungu isiyofaa

"Watu wanaozingatia miungu isiyofaa"

kukataa uaminifu wako kwa wenyewe

"wanakukataa, ambaye angekuwa mwaminifu kwao"

Jonah 2:9

Taarifa za jumla

Huu ni muendelezo wa sala ya Yona iliyoanzia 2:1

Lakini mimi

Maneno haya kwa Kiingereza yanaonyesha kwamba kuna tofauti kati ya watu Yona alikuwa amesema juu na yeye mwenyewe. Walizingatia miungu isiyofaa, lakini angependa kumwabudu Bwana. AT 'Lakini mimi'

nitakuchinjia kwa sauti ya shukrani

Hii ina maana kwamba Yona angeweza kumshukuru Mungu wakati alipomtolea dhabihu dhabihu. Si wazi kama Yona alipanga kumshukuru Mungu kwa kuimba au kupiga kelele kwa furaha.

Wokovu kutoka kwa Bwana

Hii inaweza kutafsiriwa ili jina la abstract "wokovu" linaelezewa kama kitenzi "salama." "Yahweh ndiye anayeokoa watu'"

juu ya nchi kavu

"juu ya ardhi" au "kwenye pwani"

Jonah 3

Jonah 3:1

Neno la Bwana likaja

Hii ni idiamu ambayo inamaanisha Yahweh alisema. Angalia jinsi ulivyotafasiri hii katika 1: 1. AT "Bwana alizungumza ujumbe wake' (Angalia tini_idiamu)

neno la Bwana

Hapa "neno" linawakilisha ujumbe wa Bwana. AT "ujumbe wa Bwana"

"Ondoka, uende Ninawi, mji ule muhimu"

"Nenda kwenye mji muhimu wa Ninawi"

Ondoka

Hii inarejea kuondoka

uhubiri ujumbe ule ambao nitakuagiza

"waambie watu kile ambacho nimekwambia uwaambie"

Basi Yona akaondoka akaenda Ninawi kwa kutii neno la Bwana

"Wakati huu Yona alimtii Bwana na kwenda Ninawi"

Basi Yona akaondoka

"Basi Yona akaondoka pwani." "akaondoka" ina maana ya kuondoka mahali Yona alikuwapo.

Sasa

Neno hili linatumiwa hapa kuashiria mabadiliko kutoka kwenye hadithi hadi habari kuhusu Ninawi.

moja kati ya safari ya siku tatu

"mji wa safari ya siku tatu". Mtu alipaswa kutembea kwa siku tatu ili apite kabisa.

Jonah 3:4

baada ya safari ya siku akapaza sauti

Inawezekana maana ni 1) "baada ya Yona kutembea safari ya siku alipaza sauti" au 2) "wakati Yona alipokuwa akitembea siku ya kwanza, alipaza sauti."

baada ya safari ya siku

"baada ya kutembea kwa siku." Safari ya siku ni umbali ambao watu huenda kusafiri kwa siku moja. AT "baada ya Yona kutembea kwa siku moja"

alipaza sauti na kusema

"alihubiri" au "alipaza sauti"

siku arobaini

siku 40" (Angalia: tafasili ya namba)

Wote hwakavaa nguo za magunia

Kwa nini watu kuvaa magunia wanaweza kuelezwa wazi zaidi. AT 'Pia huvaa kitambaa kikubwa ili kuonyesha kwamba walikuwa na huruma kwa kuwa wamefanya dhambi' (UDB) (Angalia tini_izo wazi)

kutoka aliyemkubwa hata mdogo.

"kutoka kwa walio wa muhimu zaidi hata wasio na umuhimu" au "ikiwa ni pamoja na watu wote muhimu na watu wote wasiomuhimu" (UDB)

Jonah 3:6

habari

"ujumbe wa Yona"

Akasimama kutoka kiti chake cha enzi

Aliinuka kutoka kiti chake cha enzi' au 'Alisimama kutoka kiti chake cha enzi.' Mfalme alitoka kiti chake cha enzi kuonyesha kwamba alikuwa akifanya kwa unyenyekevu.

kiti cha enzi

Kiti cha enzi ni kiti ambacho mfalme anakaa. Inaonyesha kwamba yeye ni mfalme.

Alitoa tangazo ambalo lisemalo

"Alitoa tamko rasmi ambalo alisema" au "aliwatuma wajumbe wake kutangaza kwa watu wa Ninawi"

wakuu

"washauri" (UDB). Hawa walikuwa watu muhimu ambao walimsaidia mfalme kutawala mji.

ng'ombe wala kundi

Hii inahusu aina mbili za wanyama ambazo watu hutunza. AT "ng'ombe au kondoo"

Wao wasile wala kunywe maji.

"Hawapaswi kula wala kunywa chochote." Sababu ambayo hawakula au kunywa chochote inaweza kuwa wazi kwa kuongeza "ili kuonyesha kuwa ni msamaha kwa dhambi zao."

Jonah 3:8

Taarifa za jumla

Huu ni muendelezo wa kile Mfalme aliwambia watu wa Ninawi.

Lakini wote

"wote"

Lakini watu na wanyama wawe wamefunikwa kwa magunia

Hii inaweza kuelezwa katika fomu ya kazi. AT "waache watu na wanyama huvaa magunia" au "waache watu na kujifunika wenyewe na wanyama wao kwa magunia"

wanyama

Neno "mnyanya" inatambulisha wanyama ambao watu wanafuga.

kulia kwa sauti kuu kwa Mungu

"ombe kwa bidii kwa Mungu." Walipaswa kuomba kwa ajili yao inaweza kuwekwa wazi. "Kulia kwa sauti kubwa kwa Mungu na kuomba huruma"

udhalimu uliyopo mikononi mwake

Hii inamaanisha "mambo ya kidhalimu aliyofanya"

Nani ajuae?

Mfalme alitumia swali hili la kuvutia ili kuwafanya watu kufikiri juu ya kitu ambacho hawangeweza kufikiri iwezekanavyo, kwamba kama watakapoacha kutenda dhambi, Mungu hawezi kuwaua. Inaweza kutafsiriwa kama taarifa 'Hatujui.' Au inaweza kuelezwa kama neno na kuwa sehemu ya hukumu ijayo "Labda."

Mungu anaweza kurejea na kubadili mawazo yake

"Mungu anaweza kufanya kitu tofauti" au "Mungu hawezi kufanya kile alichosema atafanya"

tusiangamie

"hatutakufa." maangamizi yake ni sawa na kuozea baharini.

Jonah 3:10

Mungu akaona yale waliyoyafanya

"Mungu alielewa kuwa waliacha kufanya vitendo mabaya"

wakaziacha njia zao mbaya

Mwandishi anazungumzia watu wameacha kutenda dhambi kama wamegeukia kwenye kitu.

Mungu alibadili mawazo yake juu ya adhabu aliyowaambia angewafanyia,

"Mungu alibadili mawazo yake juu ya adhabu aliyowaambia angewafanyia" au "Mungu aliamua kuwaadhibu kama alivyosema"

nae hakufanya hivyo

Nini Mungu alipaswa kufanya inaweza kufanywa wazi. AT "na hakuwaadhibu' au 'na hakuwaangamiza"

Jonah 4

Jonah 4:1

Eh, Bwana

Neno "Eh" linaelezea hisia ya Yona ya kuchanganyikiwa.

haya sio yale niliyosema wakati niliporudi katika nchi yangu

Yona alitumia swali hili la kumwonyesha Mungu jinsi alivyo hasira. Pia, kile Yona alisema wakati aliporudi katika nchi yake mwenyewe inaweza kuelezwa waziwazi. AT "Nilipokuwa bado katika nchi yangu nilijua kwamba kama nitawaonya watu wa Ninawi, watajibu, na huwezi kuwaangamiza"

Nilifanya kwanza na kujaribu kukimbia Tarishishi

Inawezekana maana ni 1) 'Nilijaribu kuzuia hili kwa kukimbilia Tarshishi' au 2) 'Nilifanya haraka na kujaribu kukimbia Tarshishi' au 3) 'Nilifanya yote niliyoweza kukimbia Tarshishi.'

wingi katika uaminifu

"mwaminifu sana" au "unapenda watu sana" (UDB)

unaghairi kutuma maafa

Hii inamaanisha 'unasema kuwa utapeleka maafa juu ya wenye dhambi, lakini kisha usiamua.' AT 'unaamua kuwaadhibu watu ambao wanafanya dhambi'

uniondoe uhai wangu

Sababu ya Yona ya kutaka kufa inaweza kuelezwa waziwazi. AT "kwa vile hutaangamiza Ninawi kama ulivyosema ungependa, tafadhali niruhusu nifariki" (UDB)

kwa maana ni bora kwangu kufa kuliko kuishi

"Ningependa kufa kuliko kuishi" au "kwa sababu nataka kufa. Sitaki kuishi "

Jonah 4:4

ni vema kwamba umekasirika?

Mungu alitumia swali hili la kuvutia ili kumwambia Yona kwa kuwa hasira juu ya kitu ambacho hakuwa na hasira juu yake. AT "Hasira yako si nzuri."

alitoka nje ya mji

ametoka mji wa Ninawi

mji utakuwaje

"nini kitatokea kwenye mji" (UDB). Yona alitaka kuona kama Mungu angeuharibu mji au hatauharibu.

Jonah 4:6

juu ya Yona ili uwe kivuli juu ya kichwa chake

"juu ya kichwa cha Yona kwa kivuli"

ili kupunguza dhiki yake

"kumlinda Yona kutokana na joto la jua"

Lakini Mungu aliandaa mdudu

"Mungu alimtuma mdudu" (UDB)

Alishambulia mmea

"Mdudu hutafuta mmea"

mmea ukapooza

Mmea ukakauka na kufa. AT: "mmea ukafa"

Jonah 4:8

Mungu aliandaa upepo mkali wa mashariki

Mungu alisababisha upepo mkali kutoka mashariki ili kumpiga Yona. Ikiwa upepo unaweza kumaanisha upepo baridi au baridi basi unaweza kujaribu hii. AT 'Mungu alimtuma joto la moto sana kutoka mashariki hadi Yona

jua lilipiga chini

"jua lilikuwa kali sana"

kichwa cha Yona

Yona anaweza kuwa amehisi joto kali juu ya kichwa chake. AT "juu ya Yona"

akaanguka

"akawa dhaifu sana" au "alipoteza nguvu zake"

Ni bora kwangu kufa kuliko kuishi

"Ningependa kufa kuliko kuishi" au "Kwa sababu nataka kufa. Sitaki kuishi. "Tazama jinsi ulivyotafasiri hii katika 4 1.

ni vema wewe kuwa na hasira juu ya mmea?

Mungu anamjaribu Yona kwa kuwa na hasira kwamba mmea umekufa na bado Mungu alitaka kuwaua watu wa Ninawi. AT "Hasira yako juu ya mmea kufa sio nzuri."

Ni vyema kuwa nimekasirika hata kufa.

"Ni vizuri kwamba nina hasira. Sasa nimekasirika hata kufa! " (UDB)

Jonah 4:10

Bwana akasema

"Bwana akamwambia Yona"

haikunipassa kuuhurumia Ninawi, mji mkuu, ...Ng'ombe?

Mungu alitumia swali hili kusisitiza madai yake ya kwamba anapaswa kuwa na huruma juu ya Ninawi. AT 'Mimi hakika ni lazima nipate huruma kwa Ninawi, mji ule muhimu ... ng'ombe.' (Angalia tini_kutaja)

ambayo kuna zaidi

Hii pia inaweza kuwa mwanzo wa sentensi mpya. AT "Kuna zaidi" au "Ina zaidi"

watu mia moja na Ishirini elfu

Watu 120,000

ambao hawajui tofauti kati ya mkono wao wa kulia na mkono wao wa kushoto

Hii inaweza kuwa njia ya kusema "hawawezi kuelewa tofauti kati ya zuri na baya."

na pia Ng'ombe wengi

Mwandishi anaelezea ukosefu wa toba ya Ninawi kwa kiasi ambacho Bwana anachukua ushiriki wa wanyama katika tendo la toba

Micah 1

Micah 1:1

neno la Yahwe likanijia

"neno la Yahwe Mungu ameongea"

Yahwe

Hili ni jina la Mungu ambalo alilojifunua kwa watu wake katika Agano la Kale.

Mmorashti

Hii inamaana anatoka Morashti ambao ni mji katika Yuda.

katika siku za Yotahamu, Ahazi, na Kezekia, wafalme wa Yuda

"wakati Yotahamu, Ahazi, na Hezekia walipokuwa wafalme wa Yuda"

lile neno aliloliona kuhusiana na Yerusalemu

"Ono aliloliona kuhusiana na watu wa Samaria na Yerusalemu"

Micah 1:2

Maelezo ya jumla:

Inazungumzia kuhusu hukumu juu ya Samaria.

Sikilizeni, ninyi watu wote. Sikilizeni Dunia, na vyote vilivyomo ndani yako

Sentensi zote hizi zinamaanisha kitu kimoja na kusisitiza kwamba kila mtu aliye duniani anapaswa kusikiliza. Mika anaongea kana kwamba watu wote wa dunia walikuwa pale wakimsikiliza.

atashuka chini na kupakanyaga mahali pa juu ya ya nchi

atapaharibu mahali pa juu kabisa juu ya nchi kana kwamba alikuwa akiwakanyaga kwa miguu yake"

Milima itayeyuka chini yake; mabonde yatapasuka vipande kama mshumaa mbele ya moto, kama maji yaliyomwagika chini ya mteremko mkali.

Hii inamaana wakati Mungu atakapokuja kuziharibu madhabahu za wapagani hakuna jambo litakalomzuia.

Micah 1:5

Haya yote ni kwa sababu ya uasi wa Yakobo, na kwa sababu ya dhambi za nyumba ya Israeli

Hivi vifungu vya maneno kimsingi vinamaanisha kitu kimoja na kukazia kwamba Yahwe anatenda kwa sababu ya dhambi za falme zote mbili yaani kaskazini na kusini .

Haya yote ni

"Bwana Mungu atakuja na kuhukumu"

Je! Sababu ilikuwa nini kwa uasi wa Yakobo? Je! Haikuwa Samaria? Je! Haikuwa Samaria?

Hapa "Yakobo" anarejelea kwa ufalme wa kusini mwa Israeli. Mika anatumia maswali kuwasisitiza hao watu wa Samaria ni sababu ya Mungu kuuhukumu ufalme wa Israeli.

Je! Sababu ilikuwa nini kwa mahali pa juu pa Yuda? Je! Haikuwa Yerusalemu?

Mika anatumia maswali kuwasisitiza hao watu wa Yerusalemu ndio sababu Mungu ya kuja kuuhukumu ufalme wa Yuda.

Micah 1:6

Nitafanya

Hapa "Mimi" inarejelea kwa Yahwe.

itakanyagwa kuwa vipande vipande...itachomwa

"Nitakanyaga kuwa vipande vipande...nichoma"

Nitayavuta mawe ya jengo lake

Hapa "yeye" inarejea kwa mji wa Samaria.

Kwa kuwa zawadi zake za ukahaba amezikusanya, na malipo ya ukahaba yatarudi

Mara nyingi kuabudu sanamu pamoja na kulala na kahaba kwenye hekalu la wapagani.

Micah 1:8

Maelezo ya jumla

Mika 1:8-16 inazungumzia hukumu juu ya Yuda.

Nitaomboleza

Hapa "mimi" inamrejea Mika.

Nitaenda peku na uchi

Hii ni ishara ya maombolezo makali mno na kujitesa.

uchi

Mara nyingi, Mika hakuwa uchi mwili mzima. Alikuwa amevaa msuli.

Nitalia kama mbweha na kuomboleza kama bundi

Hawa ni wanyama wajulikanao kwa sauti na kilio chao kisichopendeza

Kwa kuwa jeraha lake haliponi

Hapa "yeye" inarejea kwa mji wa Samaria. Hii inamaana hakuna kitu kinachoweza kuzuia jeshi la adui ambalo ninalokuja kuwaharibu watu wa Israeli.

kwa kuwa imefika kwa Yuda

Hapa "hiki" inarejea kwa "jeraha," ambayo ni, kwa jeshi ambalo Mungu atakalolitumia kuiharibu Samaria.

Beth Leafra

Unaweza kutaka rejea kusema, "Jina la huu mji linamaana ya 'nyumba ya vumbi."'

Najibiringisha mimi mwenyewe kwenye mavumbi

Watu chini ya hukumu ya Mungu wanaweka wazi huzuni yao katika njia imara.

Micah 1:11

Maelezo ya Jumla:

Kwa kuwa maana za vijiji na miji, unaweza kutaka kuingiza hiyo habari katika rejea.

Shafiri

Jina la huu mji linatamkika kama maana moja "uzuri." Lipo kinyume na "Utupu na aibu."

katika uchi na aibu

Adui wa majeshi mara nyingi waliwafanya wafungwa wao kutembea uchi kabisa. Na kulikuwa na aibu katika kuanza kuwashinda watu.

Zaanani

Jina la huu mji linamaanisha "kutoka nje." Wanaogopa kutoka nje na kusaidia.

Beth Ezeli

Jina la huu linamaanisha "nyumba ya kuchukuliwa."

kwa kuwa ulinzi wao umechukuliwa

"kwa kuwa nimechukua kila kitu ambacho kingeweza kuwalinda"

Marothi

Jina la huu mji linamaanisha "uchungu."

kwa sababu janga umetoka kwa Yahwe

"Janga" ni neno la msingi katika Mika ambalo litakalojitokeza tena.

Micah 1:13

Lakishi

Kuna kucheza na neno hapa kama Lakishi inatamkika kama "kwenye magari ya farasi" katika Kiebrania. Watu wanaofungia magari ya farasi kukimbia, sio kupigana. Lakishi ilikuwa ya pili kwa Yerusalemu katika umuhimu katika Yuda.

binti Sayuni

"Binti" wa mji inamaanisha watu wa mji. Tafsiri za kubadilishana: "watu wa Sayuni wale waishio katiaka Sayuni."

kwa kuwa makosa ya Israeli yalionekana kwako

"kwa kuwa hamjatii kama watu wa Israeli walivyofanya"

Moreshethi Gathi

Unaweza kutaka kuongeza rejea kusema "Jina 'Moreshethi' maana yake 'kuondoa' na inalingana katika kutamkwa kwenye neno kwa ajili ya 'mchumba."' Iko kama Moreshethi ni bibi harusi ambaye Ashuru amchukuaye "zawadi za kuagana" ni vitu vitolewavyo na bibi harusi kwenda kwa bwana harusi. Moreshethi Gathi kilikuwa kijiji cha nyumbani kwa Mika.

Akzibu

Unaweza kuongeza rejea kusema "Jina la huu mji linatamkika karibu sawa kama Kiebrania kueleza kwa ajili ya 'kitu cha udanganyifu."'

Micah 1:15

Nitaleta tena

Hapa "mimi" inarejea kwa Yahwe.

Mareshi

Unaweza kutaka kuweka rejea kusema, "Kuna kucheza juu ya maneno hapa pamoja na jina la hiki kijiji na neno la Kiebrania kwa ajili ya 'kushinda."' Huu msemo ulitumika katika kushinda Israeli Kanaani; sasa Israeli itashinda. Hiki kijiji ni kama kilikuwa karibu na kijiji cha nyumbani kwa Mika mwa Moreshethi Gathi.

Adulamu

Hii inarejea kwa mji wa kifalme wa Wafilisti.

Nyoa kichwa chako na kata kipara

Wale waliokuwa wakinyoa kichwa ilikuwa alama ya kuomboleza kwa ajili ya Waisraeli.

Micah 2

Micah 2:1

Maelzo ya Jumla:

Sasa Mika 2:1-11, lengo liondoalomiji kuhukumiwa kwa wakuu katika Israeli ambao wanaochukulia manufaa kwa maskini na sio kufuata maagizo ya Mungu.

Micah 2:3

huu ukoo

Huu "ukoo" inaihusu jamii nzima ya Israeli, ambayo watu matajiri wanawakandamiza maskini. Dhambi za wakuu zinarudi juu ya taifa zima.

ambazo hamtazitoa shingo zenu

Yahwe inamaanisha adhabu yake ni kama nira kuzunguka shingo zao. Ni kitu ambacho kitashusha chini kiburi cha tajiri.

kuomboleza kwa maombolezo ya huzuni

"watalia kwa sauti"

Je! Ataondoaje kutoka kwangu?

adui hutumia swali katika wimbo wao kuwaelezea wakuu mshangao wa Israeli waliojisikia kwa sababu Mungu aliikuchukua nchi yao na kuitoa kwa mtu mwingine kama walivyokuwa wameochukua kutoka maskini. "Ameichukua kutoka kwangu!"

Kwa hiyo, ninyi watu matajiri hamtakuwa na uzao kugawanya eneo kwa kupiga kura katika mkutao wa Yahwe.

Wale ambao walioichukua nchi kutoka maskini hawatapokea urithi wamewakataa wengine.

Micah 2:6

Maelezo ya jumla:

Mika 2:6-11 inawatambulisha manabii ambao hawajahubiri kwa ufasaha, wale waliomkataa Mika, na njia nyingi tajiri amezitumia vibaya nguvu zao.

wanasema

"watu wa Israeli husema"

Hawatahubiri

"Manabii hawatatabiri"

Je! Roho wa Yahwe amekasirika? Je! haya ni matendo yake kweli?

Watu hutumia maswali kusisitiza kwamba hawajaelewa na kutomwamini Mungu atawaadhibu kweli.

Maneno yangu sio mazuri kwa kila mtu atembeaye kwa unyoofu?

Mika anatumia swali kuwafundisha watu. "Ujumbe wangu ni mzuri kwa wale wanaohusika kwa kufanya yale mazuri."

watu wangu

Hapa "wangu" linamrejea Yahwe.

Mmelivua joho, nguo, kutoka wale wapitao wasioshutumiwa

Maana ziwezekanazo 1) Mika anamaanisha watu matajiri waovu ni kweli wanaiba majoho kutoka maskini, lakini hii ni tofauti. Au 2) Mika anarejea kwa watunzaji wa mapato ya mawia mavazi ya nje ya maskini wajao kuazima pesa na kutoa mavazi kama dhamana warudishapo. Kulingana na sheria kwenye Kutoka, walitakiwa kurudisha kabla ya kuchwa kwa sababu inaweza kuwa jambo pekee la mtu maskini kuwekwa joto usiku

Micah 2:9

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kuongea na watu matajiri waovu katika Israeli.

mnachukua baraka zangu kutoka kwa watoto wao wadogo milele.

Hii inarejea , kwa ujumla, kwa baraka Mungu alizowawapati watu wake. Inaweza kurejea kwa 1) kuwa wamiliki wa nchi katika Israeli, 2) ahadi ya baadaye au 3) kwa mababa wa wana, wakulima waliofanya kazi kwa bidii kuanzisha taifa.

imeangamizwa kwa maangamizo kabisa

"Nitaiangamiza kabisa"

angefikiriwa

"ungemfikiria"

Micah 2:12

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kuongea. Mwishoni mwa hii sura, Yahwe anajionyesha yeye mwenyewe kuwa mchungaji ambaye awachungaye watu wake. Anaweza hasa kuwatambulisha wale walio katika Yerusalemu ambaye amerudi kutoka Ashuri.

Mtu avunjaye hufungua njia...Yahwe atakuwepo kwenye vichwa vyao.

Hii ni picha ya Mfalme akiwaongoza watu wake mbali na mji uliozungushiwa ukuta.

Micah 3

Micah 3:1

Maelezo ya Jumla:

Sura ya 3 inawalenga wakuu wapotoshaji katika Israeli.

Nimesema

Hapa "mimi" inamrejea Mika.

Je! Sio sahihi kwenu kuifahamu haki?

Mika anatumia swali kuwakemea wakuu kwa sababu hawakuwa wanawalinda watu au kuwatendea haki.

ninyi manaorarua ngozi yao, miili yao kutoka mifupa yao...kama nyama katika chungu

Mika anatumia hii picha mbaya ya bucha kuwakata wanyama kuwa nyama kusisitiza jinsi Mungu alivyo fadahaishwa na wakuu kwa sababu ya jinsi walivyo wakatili kwa wale waliotakiwa kulindwa.

Micah 3:4

Maelezo ya Jumla:

Mika anaendelea kuongea.

lia kwa Yahwe

"piga kelele kwa Yahwe kwa ajili ya msaada"

Atauficha uso wake kutoka kwenu

Hii inamaanisha Mungu hatasikia vilio vyao. Hawatasikia vilio vya maskini, na hivyo wapokee kama walivyofanya kutoka kwa Mungu.

Micah 3:5

Maelezo ya Jumla:

Mika anaendelea kuongelea hukumu juu ya manabii wa uongo.

itakuwa usiku kwenu...siku itakuwa giza juu yao

Yahwe anasema katika 3:6 hawa manabii wa uongo hawatapokea tena ujumbe wa Mungu kwa watu wa Israeli. Wakati mwingine manabii walipata ujumbe kutoka kwa Mungu kupitia maono, au ndoto usiku.

Waonaji watawekwa kuwa aibu, na waaguzi watachanganyikiwa

"Nitawafanya waonaji kuwa aibu, na nitawachanganya waaguzi"

Wote watafunga midomo yao

"Hawataongea tena"

kwa kuwa hakuna jibu kutoka kwangu

Hii inamaanisha Mungu atakuwa kimya kama sehemu ya adhabu yao.

Micah 3:8

Lakini kwangu

"Mimi" hapa inamrejea Mika, nabii wa kweli amejitenga kutoka manabii wa uongo.

Nimejaa uwezo kwa Roho ya Yahwe, na nimejaa haki na uweza

Roho wa Yahwe alichagua kumpatia Mika nguvu, haki, na uweza katika uhodari, njia ya aina yake. "Roho wa Yahwe amenijaza nguvu, haki, na uweza" au "Roho wa Yahwe amenipa nguvu, haki, na uweza"

kumtangazia Yakobo kosa lake, na kwa Israeli dhambi yake

Hivi virai vyote vinamaana moja na kusisitiza hao watu wote wa falme zote kaskazini na kusini wamefanya dhambi.

Micah 3:9

Mmeijenga Sayuni kwa damu na Yerusalemu kwa uovu

Matajiri walikuwa wakijijengea wenyewe nyumba nzuri mara nyingi kwa gharama na kuwatenda vibaya maskini.

damu

Hapa "damu" inarejea kuua.

Je! Yahwe yu pamoja nasi? Hakuna uovu utakaokuja juu yetu.

Mika anawanakuu watu wafikiriao tofauti Yahwe hatawaadhibu kwa matendo yao maovu. Neno la Kiebrania la "uovu" hapa ni sawa kama "janga" katika 2:3, neno kuu katika kitabu.

Micah 3:12

kwa sababu yenu

Hapa "ninyi" inawarejea makuhani, manabii, na wakuu wa wa mstari uliopita.

Sayuni italimwa kama shamba, Yerusalemu itakuwa rundo la kifusi, na mwinuko wa hekalu utakuwa kama mwinuko wa msitu.

Mika anamaanisha kwamba Yerusalemu itaharibiwa kabisa. Mji mkubwa pamoja na watu wengi waishio huko wakuwa wametelekezwa na kukomaa kama shamba au msitu.

Sayuni atalimwa kama shamba

Baada ya uharibifu wake, Yerusalemu atapatikana kwa kulimwa. "Watu wengine watailima Sayuni kama shamba."

na mwinuko wa hekalu utakuwa kama mwinuko wa msitu.

Hakuna hata eneo la hekalu litakaloacha kuharibiwa. Wakuu wamelipotosha, na litaharibiwa pia.

Micah 4

Micah 4:1

mlima wa nyumba ya Yahwe utakuwa imara

"Yahwe atauimarisha mlima ambapo hekalu lake lilipojengwa"

juu ya milima mingine

Hii inamaanisha Mlima Sayuni utakuwa wa muhimu zaidi ya milima yote. Pia inaweza kumaanisha kwamba huu mlima utakuwa mrefu zaidi katika dunia, sio katika eneno pekee.

utakuwa imara juu ya milima mingine

"utaheshimiwa zaidi kuliko mlima mwingine wowote"

watu watatiririka kuuendea

Watu wa mataifa wataenda kwenye mlima wa Yahwe kama mkondo utiririkiao. Hii inamaanisha kwamba watu wengi wataenda. "watu wa mataifa watatiririka kama mto kuuendea" au "watu wa mataifa watauendea"

Micah 4:2

njooni tuupande mlima wa Yahwe, kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo

Vyote mlima na nyumba ni kumbukumbu kwa hekalu la Yerusalemu.

Atatufundisha njia zake, na tutaenenda katika njia zake

Hapa "njia zake" na "njia zake" zinarejea kwa kile ambacho Mungu ataka watu wakifanye. Pia, "kuenenda" maana yake watatii kile asemacho.

Kwa kuwa kutoka Sayuni sheria itatoka, na neno la Yahwe kutoka Yerusalemu

Hapa maneno "sheria" na "neno" yanazungumzia jambo moja. Mataifa ya dunia watasikiliza sheria ya Mungu katika Yerusalemu.

plau

Plau ni kengee ambayo watu hutumia kulimia kwenye udongo ili wapande mbegu.

Watazipiga panga zao kwenye plau na mikuki yao kuwa miundu ya kupogolea

Virai hivi vyote vinamaanisha kwamba watarudisha silaha zao za vita kwenye vifaa watakavyovitumia kuandalia chakula.

miundu ya kupogolea

Mundu wa kupogolea unatumika kukatia matawi au au visiki kutoka kwenye mmea kuufanya uzae vema.

Micah 4:4

Maelezo ya Jumla:

Mika anaendelea kuelezea "siku za mwisho" wakati watu watakapojifunza na kuitii sheria ya Yahwe.

chini ya mzabibu na chini ya mtini wake

Hii ni picha ya watu waishio katika amani.

kwa kuwa kinywa cha Yahwe wa majeshi kimenena hivi

"kwa kuwa Yahwe wa majeshi amenena"

enenda...katika jina la

Hiki kirai kinamaanisha kuabudu na kutii

Micah 4:6

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaelezea "siku za mwisho" wakati watu watakapojifunza na kutii sheria ya Yahwe.

Siku hiyo

"Katika siku zijazo"

Nitamkusanya achechemeaye

"Nitawaleta pamoja wale ambao ni wadhaifu"

na kumkusanya aliyefukuzwa

"na kuwakusanya wale ambao nimewafanya kuwatoka"

na wale waliotupwa mbali kwenye kwenye taifa imara

"na wale niliowatupa mbali nitalifanya taifa imara"

mnara wa saa kwa ajili ya kundi

Yahwe anatumia hiki kirai kusisitiza kwamba watu wa Yerusalemu walitakiwa kuulinda na kuuangalia kwa ajili ya watu wengine wa Israeli.

kilima cha binti Sayuni

"Binti" wa mji inamaanisha watu wa mji. "kilima ambacho watu wa Sayuni huishi"

kilima

Baadhi ya matoleo ya kisasa yanaelewa hili neno la Kiebrania kumaanisha "boma" au "ngome" hapa.

Micah 4:9

Sasa, kwa nini unapiga kelele kwa sauti kuu?

Mika anawatania watu, kujaribu kuwafanya kufikiria kuhusu kwa nini Mungu anashughulika nao katika njia hii. "Sasa, unapiga kelele kwa sauti kuu."

Je! Hakuna mfalme miongoni mwenu? Je! Mshauri wako amekufa? Je! Hii ndiyo sababu uchungu umekushika kama yule mwanamke katika kuzaa?

Mika anaendelea kuwahutubia watu katika sauti ya mzaha. Jibu la haya maswali ni hapana. Mfalme na washauri bado wapo huko, lakini wako kama hawana maana na wasio na matumaini. "Hivyo kwa nini unaomboleza sasa? Je! Ni kwa sababu hauna mfalme? Je! watu wako wenye hekima wamekufa? Unalia kwa sauti kuu kama mwanamke anayezaa mtoto."

Kuwa katika uchungu na kuzaa, binti wa Sayuni, kama mwanamke mwenye uchungu

Mika anatumia picha ya mwanamke katika kuzaa kusisitiza masumbuko makali ya uhamishoni. Anamaanisha kwamba watakuwa katika uchungu kwa sababu Mungu anawaadhibu kwa kuwapeleka mbali na Israeli. Wengi wao hawatakuja nyumbani tena.

Huko utaokoka. Huko Yahwe atakuokoa

"Huko Yahwe atakuokoa"

Micah 4:11

Maelzo ya Jumla:

Yerusalemu itawashinda maadui zake.

Acha atiwe unajisi; acha macho yetu yaitazame Sayuni

"Ngoja tuuangamize mji wa Yerusalemu na kuwaharibu watu wake hivyo tunaweza kuchukua furaha kubwa katika kuanguka kwao."

kwa kuwa amewakusanya kama miganda kupura sakafuni

Hii inamaanisha pia Mungu anajiandaa kuwaadhibu watu wa mataifa.

Micah 4:13

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaonyesha picha ya kupuria sakafu.

Inuka na pura, binti Sayuni

Mungu atawatumia watu wa Sayuni kuwaadhibu watu wa mataifa.

Nitaifanya pembe yako kuwa chuma, na nitazifanya kwato zako kuwa shaba

Yahwe anawalinganisha watu wa Sayuni na ng'ombe shujaa ambaye angepura ngano. Hii inamaanisha Yahwe atawafanya watu wa Israeli hodari tena ili waweze kuwashinda mataifa mengine.

Micah 5

Micah 5:1

kundi la watu, watu, watu, watu, watu

Neno "watu" au "kundi la watu linarejea kwa kundi la watu ambao wanatumia lugha moja wote na utamaduni mmoja. Kirai "watu" mara nyingi inarejea kwa mkusanyiko wa watu katika mahali fulani au katika tukio maalumu.

Yerusalemu

Yerusalemu ilikuwa asili ya mji wa Wakanaani ambao badaye ulikuwa mji muhimu zaidi katika Israeli. Inaonyesha kama kilomita 34 magharibi mwa Bahari ya Chumvi na kaskazini mwa Bethelehemu. Bado ni mji mkuu wa Israeli ya sasa.

Israeli, Waisraeli, taifa la Israeli

Neno "Israeli" ni jina ambalo Mungu alimpatia Yakobo. Maana yake, "alipambana na Mungu."

ufito

Neno "fimbo" linarejea kwa nyembamba, ngumu, fimbo kama kifaa ambacho kilitumika katika njia nyingi tofauti tofauti. Ilikuwa kama walau mita moja katika urefu.

Micah 5:2

Lakini wewe, Bethelehemu Efrata

Yahwe anazungumza na watu wa huu mji kana kwamba wako pale wanasikiliza.

Efrata

Hili ni mojawapo ya jina la eneo ambalo Bethehemu ilipokuwa au inaitwa kwa jina jingine kwa ajili ya Bethelehemu au inatofautisha Bethelehemu hii kutoka nyingine. Bethelehemu ipo kama maili sita kusini mwa Yerusalemu. Palikuwa ni nyumbani mwa mji wa Mfalme Daudi. Watafsiri wanaweza kuongeza hii rejea: "Jina 'Efrata' maana yake 'kuzaa matunda."'

hata kama uko mdogo katikati ya koo za Yuda

Hii inamaanisha Mungu atafanya mambo makubwa kupitia kidogo na mji usiokuwa na maana.

atakuja kwangu

Hapa "mimi" inamrejea Yahwe.

ambaye mwanzoni ni kutoka nyakati za kale, kutoka milele

Hii inaurejea ukoo mtawala kutoka familia ya zamani ya Mfalme Daudi. Virai "kutoka nyakati za zamani" na "kutoka milele" kimsingi inamaanisha kitu kimoja na kusisitiza jinsi hii safu ya familia ilivyo ya zamani.

Kwa hiyo Mungu atawatoa

"Kwa hiyo Mungu atajitenga na watu wa Israeli"

hadi wakati yeye aliye katika uchungu atakapozaa mtoto

Hii inarejea kipindi wakati mtawala amezaliwa, muda wenye ukomo.

mabaki ya ndugu zake

"mabaki ya jamaa zake Waisraeli." Hawa ni Waisraeli katika uhamisho. Hapa "yeye" inamrejea mtoto ambaye atakuwa mtawala.

Micah 5:4

Maelezo ya Jumla:

Hii mistari inaendelea kumwelezea mtawala kutoka Bethelehemu.

Atasimama na kulichunga kundi lake kwa nguvu za Yahwe

"Atawaongoza watu wake katika nguvu ya Yahwe."

katika ukuu wa enzi ya jina la Yahwe Mungu wake

"katika mamlaka ya nguvu ya Yahwe Mungu wake"

Watabaki

Hapa "wao" inawarejea watu wa Israeli. Neno "Israeli" au "Yerusalemu" imehusika. "Watu watabaki Israeli" au "Watu watabaki katika Yerusalemu"

kwa kuwa atakuwa mashuhuri hata mwisho wa dunia

Hii inamaanisha kwamba mbeleni watu wote kutoka kila taifa watatoa heshima kwa mtawala wa Israeli.

Atakuwa amani yetu

Hapa "yetu" inamrejea Mika na watu wa Israeli. "Atakuwa mtu wa amani"

wachungaji saba na viongozi saba juu ya watu

Hapa "wachungaji" inamaanisha "watawala." pia, unaweza kutaka kuongeza rejea inayosema, "Hesabu 'saba' na 'nane' zimeunganishwa kumaanisha kwamba zitakuwa zaidi za kutosha viongozi kukutana na hitaji."

Micah 5:6

Wataichunga nchi ya Ashuru

Hapa kuwashinda Waashuru inzungumziwa kana kwamba ilikuwa kuwachunga kondoo.

nchi ya Nimrodi

Hili ni jina jingine kwa nchi ya Ashuru. Nimrodi alikuwa muwindaji na kiongozi wa mwanzoni. Watafsiri wanaweza kuongeza hii rejea: "Jina 'Nimrodi' maana yake 'uasi.'"

katika malango yake

Hii sura inaweza kueleweka kama "katika malango yake." Malango ya mji yalikuwa kwenye maeneo ya watu wengi ambapo mara nyingi wakuu walifanya maamuzi muhimu.

Ataokoa

"Mtawala ataokoa"

kama umande utokao kwa Yahwe, kama manyunyu kwenye majani

Hii inasisitiza kwamba watu wa Yuda watakuwa wakijifurahisha, baraka, kwa mataifa.

ambayo hayamsubiri mtu, na hayawasubiri wana wa mwanadamu

"na watasubiri kwa na kumtegemea Mungu"

Micah 5:8

katikati ya mataifa, katikati ya watu wengi

Hivi virai viwili kimsingi vinamaanisha jambo moja na kusisitiza kwamba "mabaki ya Yakobo" wataishi katika mataifa mengi tofauti tofauti.

kama simba katikati ya wanyama wa msitu, kama mwana simba katikati ya kundi la kondoo. Wakati akipita katikati yao, atawakanyaga juu yao na kuwararua kuwa vipande vipande

Hii inasisitiza kwamba watu wa Israeli watakuwa na uwezo na ujasiri wakiwa uhamishoni kuhukumu na kuwaharibu maadui zao.

Micah 5:10

Itatokea siku hiyo

Hii inarejea kwa mda usio dhahiri mbeleni, ni kama kipindi cha uhamisho.

Nitawaharibu farasi wako kutoka miongoni mwenu na nitayavunja magari ya farasi

Watu wa Israeli walitumia farasi na magari ya farasi tu katika vita. Pia ilijumuisha ushirikiano na wageni, nchi zisizomjua Mungu. Mungu hakutaka watu waamini silaha zao za vita kuwalinda zaidi kuliko walivyomwamini yeye.

Micah 5:12

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kuongea na watu wa Israeli.

Micah 6

Micah 6:1

Inuka na ueleze kesi yako...atapigana katika mahakama juu ya Israeli

Katika 6:1-5 Mika anatumia chumba cha mahakam kama picha. Yahwe anazungumza mbele ya mashahidi kuelezea kwa nini watu wa Israeli wamemwacha mungu na kuanza kuabudu sanamu.

milima...vilele...mivumilivu ya dunia

Mika anaongea na hivi vitu kana kwamba ni wanadamu. Mika anatumia milima, vilele, na misingi ya dunia kama ushahidi wa milele juu ya kuabudu sanamu za watu wake.

Micah 6:3

Maelezo ya Jumla:

Hii inaendelea madai ya Yahwe juu ya watu wa Israeli.

Watu wangu, nimefanya nini kwenu? nimewachosha mara ngapi? shuhudieni dhidi yangu!

Mungu anatumia haya maswali kusisitiza kwamba yeye ni Mungu mwema, na hajafanya kitu kuwafanya watu kukoma kumwabudu yeye. "Watu wangu, nimekuwa mwema kwenu. Sijafanya kitu kuwafanya mnichoke. Kama mnafikiri nimefanya, shuhudieni juu yangu, sasa."

nyumba ya utumwa

"mahali ambapo mlipokuwa watumwa"

kumbukeni

"kumbuka"

Balaki mfalme wa Moabu alivyotunga, na vile ambavyo Balamu mwana wa alivyomjibu

Hii inaonyesha kwenye tukio la nyuma wakati Mfalme Balaki alipompangisha Balamu kuwafanya watu wa Israeli. Aidha, Mungu alimruhusu Balamu kuwabariki watu tu.

Beori

Hili ni jina la baba yake na Balamu.

Shitimu

Hili ni jina la mahali katika Moabu.

kwamba mnaweza kujua matendo ya haki yangu, Yahwe.

"hivyo basi mnaweza kukumbuka mimi ni nani, na nini nimefanya juu yenu"

Micah 6:6

Je nilete nini kwa Yahwe, ninapoenda kumwinamia Mungu aliye juu? Je ninaweza kuja kwake na sadaka za kuteketeza, pamoja na ndama wenye mwaka mmoja?Je Yahwe atapendezwa na maelfu ya kondoo waume, au na elfu kumi za mito ya mafuta? Je nimtoe mzaliwa wangu wa kwanza kwa ajili ya kosa langu, tunda la mwili wangu kwa ajili ya dhambi yangu mwenyewe?

Mika anatumia maswali kuwafundisha watu wa Israeli kusu kile hasa kinachomtukuza Mungu. "Hakika hufikirii kwamba unaweza kumtukuza Mungu kwa kumletea ndama mkubwa mwenye mwaka mmoja, kondoo 1,000, 10,000 mito ya mafuta, au mtoto wako wa uzao wa kwanza kama sadaka kwa ajili ya dhambi zako."

mzaliwa wangu wa kwanza kwa ajili ya kosa langu, tunda la mwili wangu kwa ajili ya dhambi yangu mwenyewe

Hivi virai viwili vinamaanisha kitu kimoja.

Amekwambia

"Yahwe amekwambia"

Micah 6:9

Sauti ya Yahwe inatangaza kwenye mji

"Yahwe anawatangazia watu wa Yerusalemu"

hata hivyo hekima hukiri jina lako

"na mtu mwenye hekima atamuogopa Yahwe" au "na mtu mwenye hekima atatii kile Yahwe asemacho"

Kuwa tayari kwa ajili ya fimbo, na kwa yule aliyeiweka

Hapa "fimbo" inarejea kwa adui askari ambaye Yahwe atawaadhibu watu wake.

kipimo cha uongo

Hii inataja mizani isiyopima vitu kwa usahihi hivyo mtu anaweza kuwaibia wengine kwa madhumuni na kutengeneza pesa nyingi zaidi kwa ajili yake mwenyewe.

Micah 6:11

Ningeweza kumfikiria mtu kuwa hana hatia kama anatumia kipimo cha ulaghai, pamoja na mfuko wa kipimo cha udanganyifu

Yahwe anatumia swali kusisitiza kwamba anaangalia hatia ya mtu adanganyaye wengine ili kutengeneza pesa zaidi. "Hakika nitamwangalia mtu mwenye hatia kama akitumia kipimo kisicho haki na uzito ili kuwadanganya wengine na kutengeneza pesa zaidi kwa ajili yake mwenyewe.

Watu matajiri wamejawa udhalimu

"Watu matajiri wanawachukulia maskini faida"

makazi yao yamesema uongo, na ulimi wao katika midomo yao unaudanganyifu

Vishazi hivi vyote vinamaanisha kitu kimoja na vimeungana kwa ajili ya msisitizo. "Ninyi nyote ni waongo." Hii itafanya matokeo ya mhemko kwa wasomaji.

Micah 6:13

Kwa hiyo nimekupiga kwa pigo linaloumiza...lakini hutakunywa divai

Yahwe anaelezea adhabu yake ya watu wake kama kumruhusu adui askari kuja na kuchukua kila kitu walichokuza, andaa, na kutunza kwa ajili yao wenyewe.

Micah 6:16

Maelezo ya jumla:

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Kanuni zilizotengenezwa na Omri zimetunzwa

"Mmefanya kile ambacho Omri alichoamuru"

Omri...Ahabu

Hawa watu wote walikuwa wafalme juu ufalme wa kaskazini mwa Israeli. Mungu aliwahesabu wote kuwa waovu sana.

Mnatembea kwa ushauri wao

"mmefanya mambo maovu ambayo Omri na Ahabu waliwaambia watu kufanya.

jambo la kuzomea

Hicho ni, kitu cha kudhihaki kwa kuzomea kwacho.

Micah 7

Micah 7:1

Kwangu mimi ni kama msimu wa mavuno...matini ya malimbuko

Mika anasisitiza kwamba hakuna tean watu waadilifu, waaminifu kwa Mungu, katika Israeli. "Kwangu mimi watu wa Israeli ni kama shamba la mzabibu baada ya mavuno na kukusanya. Mizabibu imejifunua. Siwezi kupata tunda lolote, lakini bado natamani sana kula tini lililoiva.

Watu waaminifu wamepotelea...kwa wavu

Mika anakuza kuonyesha jinsi ambavyo hali ilivyo mbaya. Anahisi hakuna mtu mwema aliyebaki katika Israeli.

Micah 7:3

Maelezo ya Jumla:

Mika anaendelea kuongea kuhusu watu wa Israeli.

Mikono yao ni mizuri mno

"Watu ni wazuri sana"

Mtu bora kwao ni kama mitemba, mwadilifu sana ni kama miche ya miba

Hii inamaanisha kwamba hata kiongozi mzuri katika Israeli amesababisha maumivu na walikuwa hawafai kitu

Imefika siku iliyosemwa nyuma na walinzi, siku ya adhabu

Hapa "yako" bado inawarejea watu wa Israeli. "Manabii wao wamewaambia kwamba Yahwe angewaadhibu"

Sasa ni muda wa machafuko yao

Hii inaweza kurejea kushinda vita. "Sasa iko hapa, na hawataelewa nini kinaendelea"

Micah 7:5

Maelezo ya jumla:

Mika anaendelea kuongea na watu wa Israeli.

Msimwamini kila jirani...watu wa nyumba yake mwenyewe

Mika anaendelea kuonyesha kwamba hakuna mtu yeyote mzuri, mwadilifu, na mwaminifu kwa Mungu miongoni mwa watu wa Mungu. Hapa anasisistiza kwamba hawawezi hata kuwaamini marafiki au familia.

Micah 7:7

Lakini kama kwangu mimi

Hapa "mimi" inamrejea Mika

Usifurahi juu yangu

Mika harejelei kwake pekee. Anamaanisha adui hatakiwi kufurahi juu ya kilichotokea kwa watu wote wa Israeli.

Wakati nitakapokuwa nimekaa katika giza, Yahwe atakuwa nuru kwangu

Mika anarejea kwenye janga ambalo linakuja kwa watu wa israeli kama "giza." Anamaanisha ingawa Mungu atamwacha adui kuja kuwaharibu sasa, atakuja kuwaokoa mbeleni.

Micah 7:9

Kwa sababu nimetenda dhambi

Mika hajirejei yeye pekee. Anamaanisha watu wote wa Israeli wametenda dhambi.

hata niteteapo kosa langu, na kutekeleza hukumu kwa ajili yangu

Hii inarejea wakati Mungu aamuapo amewaadhibu watu wake mno. Kisha atawaadhibu watu wa mataifa mengine ambao waliowajeruhi watu wa Israeli.

Atanileta kwenye nuru

" Atakuja na kutuokoa kutoka maadui zetu. Itakuwa kama kumleta mtu katika giza kwenye nuru"

Micah 7:10

Kisha adui yangu

Mika hajirejei yeye pekee. Anamaanisha adui wa watu wote wa Israeli.

Yuko wapi Yahwe Mungu wako?

adui hutumia swali kuwatania watu wa Israeli. "Yahwe Mungu wako hawezi kukusaidia"

Macho yangu

"Mimi" au "sisi"

yatamtazama yeye

Hapa "yeye" inawarejea maadui ambao waliowajerui watu wa Israeli.

atakanyagwa chini

"maadui zao watawakanyaga chini"

Micah 7:11

Siku ya kujenga kuta zako zitakuja

Hapa "kuta" inarejea kwa kuta kuzunguka miji yao, ambzo zimeandaa usalama na ulinzi kutoka maadui zao.

mipaka itasogezwa mbali sana

"Yahwe ataisogeza mipaka ya ukubwa wa nchi yenu" au "Yahwe ataongeza ukubwa zaidi wa ufalme wenu"

Hizo nchi zitakuwa zitakuwa zimejitenga

"Zile nchi zitakuwa tupu" au "Hakuna atakayeishi katika hizo nchi"

Micah 7:14

Chunga watu wako kwa fimbo yako, kundi la urithi wako

Mika anaomba kwa Yahwe, akimuuliza kuwalinda watu wake wa Israeli tena. Hapa "fimbo" inawarejea wakuu wa Mungu na kuongoza, kama mchungaji atumiavyo fimbo kuongoza na kuzilinda kondoo zake.

Wanaishi wenyewe kwenye msitu

Mika anamaanisha kwamba baadhi ya watu wanaishi ambapo aridhi ni maskini na wamejitenga na hawawezi kujipatia bidhaa zinazohitajiaka.

Waache wachunge katika Bashani na Gileadi

Hii mikoa inajulikana kama nchi tajiri kwa kukuza chakula. Hivyo Mika anauliza upanuzi zaidi wa eneo, ambalo lilikuwa limepotea kwa wavamizi miaka ya nyuma.

kama siku za zamani

Hii inaweza kurejewa wakati Suleimani alipokuwa mfalme.

Nitaonyesha

Hapa "mimi" inamrejea Yahwe.

Micah 7:16

Wataweka mikono yao juu ya midomo yako; masikiio yao yatakuwa kiziwi

Hii inaonyesha jinsi walivyo na hofu, sana hivyo hawawezi kujibu.

Watalamba vumbi kama nyoka, kama viumbe vitambaavyo juu ya nchi

Virai vyote vinamaanisha jambo moja. Maadui wa Mungu wataaibishwa kabisa na kuja kwake katika hofu baada ya kuona mambo yenye nguvu ayafanyayo.

Micah 7:18

Ni nani aliye Mungu kama wewe

Mika anatumia swali kusisitiza kwamba hakuna mwingine afanyaye mambo ambayo Yahwe ayafanyayo.

mabaki ya mrithi wako

"wale walio wakwetu watu wako waliochaguliwa ambao walioponea chupuchupu adhabu yako"

Micah 7:19

Uta

Hapa "wewe" inamrejea Yahwe.

juu yetu

Hapa "sisi" inamrejea Mika na watu wa Isralei.

utayakanyaga maovu chini ya miguu yako. Utazitupa dhambi zetu zote kwenye vilindi vya bahari

Hii inamaanisha Mungu atazisamehe kabisa dhambi za watu na hakutakuwa tena na adhabu ya watu kwa ajili yao.

mpatie ukweli Yakobo na agano aminifu kwa Ibrahimu

Hapa "Yakobo" na "Ibrahimu," ambao ni mambabu wa taifa la Israeli, inarejea kwa watu wa Israeli sasa.

kwa babu zetu

Hii inamrejea Ibrahimu na Yakobo, na labda wengine waliokuwa hai wakati Mungu alipolifanya agano lake pamona na Israeli.

Nahum 1

Nahum 1:1

Maelezo ya jumla

Nahumu anaelezea uharibifu wa Ninawi katika shairi.

Maono kuhusu Ninawi.

Ujumbe kutoka kwa Mungu kuhusu mji wa Ninawi.

Mwelkoshi.

Mtu kutoka kijiji cha Mwelkoshi.

Nahum 1:2

Yahwe

Hili ni jina la Mungu ambalo alilifunua kwa watu wake katika Agano la Kale.

hatakuwa na namna ya kuacha kuwahesabia hatia adui zake

Hii inamaanisha kwamba Yahwe atawahukumu na kuwaadhibu adui zake wasipomtii yeye.

Nahum 1:4

Maelezo ya jumla

Nahumu anaendelea kueleza nguvu ya Yahwe juu ya dunia yote.

Milima hutetema kwenye uwepo wake, na vilima huyeyuka; dunia huanguka mbele zake

"Milima, vilima, na dunia humwogopa Yahwe"

hutetema

kama mtu ambaye ameogopa

huanguka

"hudondoka chini ya ardhi kwa woga"

Nahum 1:6

Maelezo ya jumla

Nahumu anaongea kuhusu uwezo wa Yahwe

ukali wa hasira yake

"nguvu ya hasira yake" au" kiwango (jumla au kiasi)cha hasira yake"

Ghadhabu yake imemwagwa kama moto, na miamba ameibomoa mbalimbali

kwa tafasiri nyingine ni : "humwaga hasira yake kama moto na kubomoa miamba kwa kuisambaratisha."

Nahum 1:7

boma

sehemu salama iliyojengwa kwa ajili ya ulinzi dhidi ya maadui

siku ya taabu

Wakati adui anapofanya shambulio. Kwa tafsiri nyingine: "Wakati mambo mabaya yanapotokea"

Nahum 1:9

Maelezo ya jumla

Nahumu anawaambia watu wa Ninawi jinsi ambavyo Yahwe atawashughulikia.

atakomesha

"kuacha kabisa kufanya"

taabu haitainuka mara ya pili

"Hatakushambulia kwa mara ya pili"

Watakuwa....chao

Nahumu anazungumza kwa Waisraeli kwa ufupi juu ya watu wa Ninawi.

watakuwa wamevurugika kama michongoma

"kabiliwa na matatizo mengi ambayo yatawazuia kuvamia"

wataharibiwa kabisa

Yahwe ataiharibu kabisa Ninawi yote

aliimarisha uovu

aliwahamasisha watu kufanya mambo maovu

Nahum 1:12

Maeleza ya jumla

Yahwe anazungumza kwa Waisraeli juu ya Ninawi.

Wananguvu ... watanyolewa... zao

watu wa Ninawi

hata hivyo watanyolewa

"Watakatwa." Yahwe anatumia picha ya kukata sufu kwenye kondoo kuonyesha njinsi atakavyo liharibu jeshi la Ninawi , hata kama wapo wengi.TN: " wataharibiwa "

nitaivunja ile nira ya watu kutoka kwako

TN: "nitakuweka huru kutoka ktika utumwa mwa watu hao"

nitaikata minyororo yako

"kata minyororo ambayo waliwafunga kama watumwa"

Nahum 1:14

Yahwe

"Yahwe" ni jina binafsi la Mungu ambalo alijifunua kwa Musa kwenye kichaka kilichowaka moto.

Nahum 1:15

juu ya milima kuna miguu ya mtu aletaye habari njema

"mtu analeta habari njema"

mtu mwovu

Nahumu anazungumza kwa watu wa Ninawi kana kwamba ni mtu mmoja.

ameondolewa kabisa

Nahumu anazungumza juu tukio la baadaye kana kwamba tayari limekwisha tokea.

Nahum 2

Nahum 2:1

Maelezo ya jumla:

Nahumu anaelezea uharibifu wa Ninawi katika shairi.

Yule ambaye atakuvunja vipande vipande

Ni namna ya picha ya mtu anayevunja chungu. TN: " Atakuharibu"

Yule ambaye atakuvunja

Mtu ambaye ni "Yule" hajawekwa wazi, kwa hiyo tafsiri inatumia kauli jumuishi: "mtu ambaye atakuvunja vipande vipande."

Linda kuta za mji, linda barabara, jitieni nguvu ninyi wenyewe, yakusanyeni majeshi yenu.

kujitayarisha kwa ajili vita

Linda kuta za mji

"Panga walinzi kwenye kuta kwa ajili ya kukinga"

Maana Yahwe anarejesha fahari ya Yakobo, kama fahari ya Israeli

Hii inamaana kuwa Yahwe atamfanya Yakobo na Israeli kuwa wakuu, na watu watawapenda tena.

wateka nyara

watu wanaoiba vitu kwa nguvu, mara nyingi katika vita

waliwaharibu

waliangamiza kila kitu.

kuharibu matawi ya zabibu zao

hapa taifa linaongelewa kana kwamba ni mzabibu uliolimwa. TN: " na kuling'oa taifa lenu kana kwamba ni shamba la mzabibu"

Nahum 2:3

mashujaa wake

askari wa mtu " ambaye takuvunja"Ninawi "vipande vipand":(2:1).

mivinje

aina ya mti ambao ubao wake unafaa kwa ajili ya silaha.

Magari ya vita yapo kasi kwenye mitaa

" madereva wa magari ya vita wanaendesha kwa fujo kwenye mitaa"

Yapo kama kurunzi

Hii inarejea kwenye mng'aro wa magari ya vita yanapoakisi mwanga kutoka kwenye jua.

Nahum 2:5

atakuvunja vipande vipande

rejea kwenye fasiri ya 2:1

anawaita maafisa wake

inaweza kumaanisha: 1. "anawakusanya maafisa wake" au 2. " anafikiria juu ya maafisa wake"

wana...kwao... hawa...

askari ambao wataushambulia Ninawi

katika kutembea kwao

"wanapotembea"

Nahum 2:8

nyara

Vitu vilivyoibiwa kwa nguvu, hasa katika vita.

hakuna mwisho wake

TN: "kuna kiasi kikubwa"

fahari ya vitu vyote vizuri vya Ninawi

inaweza kumaanisha: 1) "vitu tele vyote vizuri" au 2) "kiasi cha vitu vyote vizuri"

Moyo wa kila mtu unayeyuka

"Watu wote wamepoteza ujasiri wao"

Nahum 2:11

pango la simba

Ninawi inalinganishwa na pango la simba kwa sababu ni sehemu ambayo wauwaji wanaishi na sehemu ambapo wanaweka vitu walivyoiba kutoka kwa watu waliowaua.

alirarua

"kabwa" simba wameng'ata makoo ya wahanga ili kuwazuia wasipumue.

kulijaza pango lake mawindo, makao yake kwa mizoga iliyoraruliwa

Mafungu haya mawili yanasema jambo jambo moja kwa njia tofauti. Pango ni sehemu ya simba kujificha, mara nyingi huwa ni shimo.

Nahum 2:13

Tazama

"Fahamu hili"

upanga utateketeza simba wenu vijana

"askari wenu watakufa vifo si vya kawaida"

upanga

"askari mwenye upanga"

utateketeza

"kuwala wote"

simba wenu vijana

"vijana wenu wenye ubora"

Nitazuia nyara zenu kutoka kwenye nchi yenu

Neno "nyara" linarejea utajiri ambao Ninawi alipatia kutoka kwenye nchi zingine.Hii inamaanisha Yahwe ataharibu uwezo wa Ninawi wa kuiba kutoka katika mataifa mengine.

Nahum 3

Nahum 3:1

Maelezo ya jumla

Nahumu anaendelea kuelezea uharibifu wa Ninawi katika shairi ambalo lilianza kwenye 1:1.

mji uliojaa damu

Askari wa Ninawi waliwaua watu wengi. TN: "Mji unahusika juu vifo vya watu wengi"

Nahum 3:3

marundo ya maiti, mafungu makubwa ya miili; hakuna ukomo wa miili

Mwandishi anaweka mkazo wa mauaji mengi dhidi ya Ninawi ambopo jambo hili limetajwa mara tatu (3)

maiti

Miili ya watu ambao wamekufa

hakuna ukomo wa miili

"kuna idadi kubwa ya miili"

kahaba mzuri, mzoefu wa uchawi

Kama vile makahaba wanavyouza kiburudisho cha kimwili na wachawi huuza maarifa na nguvu zilizopatikana kwa miujiza, watu wa Ninawi nao huuza watu waliowachukua katika vita na kujipatia faidi kwa dhambi yao.

Nahum 3:5

Tazama

Neno hili linavuta usikivu kwa kile kinachokuja baadaye.

ni nani ataomboleza kwa ajili yake?' Ni wapi ninaweza kumpata mtu wa kukufariji?

TN: "hakuna mtu atayelia kwa ajili yake, na siwezi kupata mtu wa kumfariji."

Nahum 3:8

Maelezo ya jumla

Nahumu anaongea kwa watu wa Ninawi kana kwamba wao ndiyo mji wenyewe.

je wewe ni bora kuliko Noamoni...yenyewe?

TN: "Ninyi si bora zaidi ya Noamoni...yenyewe."

Noamoni

mji mkuu wa zamani wa Misiri, ambao Waashuru waliuteka.

ambao ulinzi wake ilikuwa bahari, ambao ukuta wake ilikuwa bahari yenyewe

Haya mafungu mawili ya maneno yana maana zenye kufanana. Maneno "bahari" yana maana ya mto Nile ambao ulitiririka karibu kwenye mji na kusababisha ugumu wa kushambuliwa.

ulinzi... ukuta

Miji ya zamani ilikuwa na "kuta" kubwa ili kuwazuia washambuliaji, na mstari wa mbele wa walinzi kuwazuia maaduai wasiufikie ukuta.

Nahum 3:10

Maelezo ya jumla

Nahumu anaongea kwa watu wa Ninawi kana kwamba wao ndiyo mji wenyewe

Lakini

Huu ni mwendelezo wa kulinganisha Ninawi na Noamoni tangu 3:8. Inaweza kumaanisha: "japo kuwa" au "hata kama"

Noamoni

mji kuu wa azamani wa Misiri, ambao Waashuru waliuteka

alikwenda...wake

Noamoni

walivunjwa vipande vipande

Wavamizi waliwaua watoto wa Noamoni kwa urahisi kama kwamba wanavunja chungu cha udongo.

walifungwa minyororo

weka katika utumwa. TN: "wakawa watumwa"

Nahum 3:12

Maelezo ya jumla

Nahumu anaongea kwa watu wa Ninawi kana kwamba wao ndiyo mji wenyewe.

Ngome

Neno hili, ambalo lingeweza kutafsiriwa kama " ngome ya jeshi" inarejea milki yote ya Ninawi na Ashuru.

Ngome zako zote zitakuwa kama mitini yenye tini zilizoiva mapema: kama zikitikiswa, zitaangukia kwenye kimywa cha mlaji

Mji wa Ninawi utachukuliwa kwa urahisi kama tunda kutoka kwenye mti.

watu miongoni mwenu ni wanawake

"watu wako ni dhaifu na hawawezi kujilinda wao wenyewe"

bawaba zake

Mihimili mikubwa ya mbao ambayo ilishikilia mageti na haikuwezekana kufungua ukiwa nje ya mji. Kuchomwa moto kwa mihimili kulifanya isiwezekane kufunga mji tena.

Nahum 3:14

Maelezo ya jumla

Nahumu anaongea kwa watu wa Ninawi kana kwamba wao ndiyo mji wenyewe.

Utateketezwa kama nzige wachanga wanavyoteketeza kila kitu

uharibifu utaharibu kama nzige wanavyoteketeza kila kitu katika njia yao.

utakuteketeza

ni "moto" au "upanga"

Ninyi wenyewe mjitengeneze kuwa wengi kama nzige wachanga, na wengi kama nzinge waliopevuka

nzinge waliopevuka-"Mujizidishe wenyewe kama tunutu! Mujizidishe wenyewe kama nzige waliopevuka!" pengine haya ni maneno ya kuanza aya mpya.

Ninyi wenyewe mjitengeneze kuwa wengi kama nzige wachanga

Maana yake watakuwa mji mkubwa sana wenye watu wengi na wataharibu nchi nyingi.

Nahum 3:16

Maelezo ya jumla

Nahumu anaongea kwa watu wa Ninawi kana kwamba wao ndiyo mji wenyewe.

Umezidisha wafanyabiashara wako zaidi kuliko nyota mbinguni

Wafanyabiashara wa Ninawi hawawezi kuhesabika kama nyota katika anga. TN:"Unawafanyabiashara zaidi kuliko uwezo wa mtu kuhesabu."

wafanyabiashara

"wachuuzi" au "watu wanaonunua na kuuza vitu"

Wafalme

Neno linalotumiwa katika siasa "Viongozi"

wakuu wenu wa majeshi

Neno linalotumiwa katika jeshi "viongozi"au mamlaka zingine za kiserikali

Nahum 3:18

wachungaji

"wachungaji" hawa ni watawala wa watu wa Ashuru.

Ni nani aliyejiepusha kwa uovu wako wa daima?

TN: "Mfululizo wa matendo yenu maovu yamewaumiza watu wengi na mataifa"

Habakkuk 1

Habakkuk 1:1

Ujumbe ambao Habakuki nabii aliuokea

Maneno haya yanatambulisha sura mbili za mwanzo wa kitabu. Kama lugha yako inahitaji sentensi kamili hapa, "Huu ni ujumbe ambao Habakuki nabii aliupokea kutoka kwa Mungu."

kwa muda gani nitalilia msaada, na hutasikia?

NI: "Nimekuwa nikilia kwaajili ya msaada kwa muda mrefu, ingawa lakini unajifanya kama hunisikii!"

Habakkuk 1:3

Taarifa kwa ujumla:

Habakuki anaendeleza maombi yake kwa Mungu.

ugomvi unainuka

"mapigano kati ya watu yanakuwa kawaida zaidi"

Uovu unawazunguka wenye haki

Hii inaweza kuwa na maana kwamba watu wenye haki wanateseka si kwa halali 1) "waovu wananguvu zaidi kuliko watu wenye haki" au 2)"kuna watu waovu zaidi kuliko watu wenye haki."

uadilifu wa uongo unaenea

NI: "uovu unatokea badala ya uadilifu" au "kukosa haki kunaongezeka"

Habakkuk 1:5

Taarifa kwa ujumla:

Yahwe anajibu maombi ya Habakuki.

Angalia mataifa na uyachunguze

"Jifunze mambo yanayoendelea katika mataifa mengine"

upana wa nchi

Hii inaweza kuwa namaana 1) kila mahali katika Yuda au 2) kila mahali duniani

nyang'anya

chukua kwa nguvu au iba kutoka kwa mmiliki halali

masikani

"nyumba"

wao ... wao ... wao wenyewe

Maaskari Wakaldayo. Mungu atainua taifa la Wakaldayo, na maaskari Wakaldayo watavamia Uyahudi.

Wanatisha na kuogofya

Maneno "kutisha" na "ogofya" kimsingi yanamaana kitu kile kile na kusisitiza kwamba kuwafanya wengine waogope sana, NI: "Wanawafanya wengine waogope sana."

endelea

"kuja"

Habakkuk 1:8

Farasi zao ... farasi zao

farasi za askari wa Wakaldayo

haraka kuliko mbwa mwitu wa jioni

Farasi za Wakaldayo wanalinganishwa na mbwa mwitu wakali ambao wanakimbilia mawindo yao wakati wa jioni wanapokuwa na njaa sana kwasababu hawajala siku nzima.

wapanda farasi wao

Askari wa Wakaldayo wanapanda farasi.

chui

kubwa, paka wepesi

wanaruka kama tai

"wapanda farasi wanaendesha kwa haraka kama tai wanavyopaa"

umati wao unakwenda kama upepo wa jangwani, na wanakusanya mateka kama mchanga

Wakaldayo ni wengi, na kama chembe chembe za mchanga upepo hubeba katika mawimbi wengi hawahesabiki, hivyo hakuna mtu anayeweza kuhesabu watu wanaokamata na kuwafanya wafungwa.

Habakkuk 1:10

Taarifa kwa ujumla:

Yahwe anaendelea kuwaeleza askari wa Wakaldayo.

upepo utatimua

majeshi ya Wakaldayo yanayovamia yanalinganishwa na upepo unaotimua kupitia upande mmoja na kwa haraka unaendelea katika eneo lingine.

Habakkuk 1:12

Taarifa kwa ujumla:

Habakuki anazungumza kwa Yahwe kuhusu Wakaldayo.

Wewe si kutoka nyakati za kale, Yahwe Mungu wangu, Mtakatifu wangu?

NI: "Wewe ni wa milelel, Yahwe Mungu wangu, Mtakatifu wangu."

wao ... wao

Wakaldayo

Mwamba

kinga ya Israeli

Waliwekwa kwaajili ya lengo la kuisahihisha Israeli

"Wao waliwekwa kwa lengo la kuisahihisha Israeli"

Habakkuk 1:13

Taarifa kwa Ujumla:

Habakuki anaendelea kuongea kwa Yahwe kuhusu Wakaldayo.

Wao ambao wanasaliti

"Wakaldayo, ambao hakuna mmoja atakayewaamini"

meza

"haribu"

kama samaki baharini ... kama vitu vitaambaavyo

Hizi kauli mbili zinadhihirisha wazo lilelile kwamba Mungu ameruhusu Wakaldayo kuwashughulikia Israeli kama viumbe wenye thamani ndogo sana, na si kama watu wanavyotakiwa kushughulikiwa.

Habakkuk 1:15

Taarifa kwa Ujumla:

Habakuki anaendelea kuongea kwa Yahwe kuhusu Wakaldayo.

ndowano ya samaki ... wavu wa samaki

vifaa vilitumika kuvua samaki

wavu

"kifaa kilitumika kuvulia "vitu vitaambaavyo"

Wanyama walionona ni sehemu yao, na nyama nene ni chakula chao

badilishana tafsiri: "wanyama wazuri sana na nyama nzuri sana ni fungu la chakula chao"

fungu

sehemu ndogo ya kitu fulani kikubwa ambacho kinatumika kati ya watu wengi

wanamaliza nyavu zao za kuvulia

wavuvi wanawamaliza samaki kwenye nyavu ili kwamba wazitupe tena na wavue samaki wengi zaidi.

Habakkuk 2

Habakkuk 2:1

mimi ... yangu ... mimi

Habakuki

yeye

Yahwe

Nitasimama katika nguzo yangu ya ulinzi na kuweka kituo changu mwenyewe juu ya mnara wa mlinzi.

Kauli hii inasema kitu kilekile kwa namna mbili tofauti. "nitazimama katika nguzo yangu juu ya mnara wa mlinzi." Habakuki anatumia kauli hii akijilinganisha yeye mwenyewe anasubiri kusikia kutoka kwa Mungu kwa askari mlinzi asimamaye kulinda juu ya mnara.

Nitageuka kuondokana na lawama zangu

Neno "geuka" linazungumzia mtu kubadilisha mawazo yake kama nikuondoka kutoka kitu kimoja kwenda kingine. NI: "Nitaacha kulaumu na kukubaliana na Mungu"

Habakkuk 2:2

Taarifa kwa Ujumla:

Yahwe anamjibu Habakuki.

Tunza maono haya, na uandike kwa dhahiri kwenye vibao

Kauli zote mbili zinasema kitu kile kile katika njia mbili tofauti. Badilisha tafsiri: "Andika kwa wazi juu vibao ambacho Mungu anakwenda kukwambia"

vibao

hivi ni vipande bapa vya mawe au udongo mfinyanzi ambao uliotumika kwaajili ya kuandika.

yule anayesoma anaweza kukimbia

Hii inaweza kumaanisha 1) mtu fulani atakimbia pamoja na vibao na kuwasomea au 2) mtu yeyote ambaye anayesoma ataweza kusoma kwa urahisi

na mwisho kuongea

kile kilichoandikwa kitatokea au kuja kuwa halisi.

na hakitakawia

Maana zinazowezekana 1) "na hakitasubiri" au 2) "na hakitakuja kwa taratibu"

Habakkuk 2:4

Taarifa kwa Ujumla:

Yahwe anaendelea kumjibu Habakuki.

Angalia!

Neno "angalia!" hapa linaongeza msisitizo kwa kile kinachofuata.

Yule ambaye anatamani hayuko sawa ndani yake ... kijana mwenye kiburi ... yeye hatastahimili, lakini hukuza hamu yake ... hukusanyika kwake mwenyewe ... anakusanyika kwaajili yake.

Yahwe anazungumzia Wakaldayo ingawa kama wako mtu mmoja. "Yeye" inarejerea kwa Wakaldayo ingawa kama wako mtu mmoja.

Hukusanya kwake kila taifa na hukusanya kwaajili yake mwenyewe watu wote.

Hapa kinasemwa kitu kimoja katika namna mbili tofauti. "Anawakusanya watu wote kutoka kila taifa" (Angalia:

Kusanya

leta pamoja

kila ... wote

idadi kubwa sana

Habakkuk 2:6

Taarifa kwa Ujumla:

Yahwe anaendelea kumjibu Habakuki. Ingawa narejerea kwa Wakaldayo kama wako mtu mmoja.

Kwa muda gani utaongeza uzito wa dhamana uliyochukua?

"Kwa wakati fulani utakuwa huwezi kuchukua dhamana kutoka kwa watu." Hii inaweza kumaanisha 1) Wakaldayo wanafanana na wanyang'anyi waliobeba dhamana wamewalazimisha watu wengine kutia saini au 2) Yahwe anatunza adhabu kwamba Wakaldayo wameiba na siku fulani atawahitaji kuwajibika.

dhamana

ahadi ya kuzingatia imetolewa kwaajili ya deni ambalo linadaiwa, daima iliandikwa kwenye udongo wa mfinyanzi

wale watakao kuwa wakikudai hawatainuka kwa ghafula, na wanaokusumbua kuamka

swali hili linaulizwa ili kwamba kuwafanya Wakaldayo wafikiri kuhusu jibu. "Wale ambao wanakukasirikia watakuja kinyume chako, wale unaowaogopa wataanza kushambulia"

wale wanaodai kwako

Nahau hii inamaanisha wale ambao wanakudeni kwamba lazima walipe. Hivyo, baadhi ya tafsiri za kisasa hutafsiri kauli hii kumaanisha wanaodai, siyo wanaodaiwa.

wale wanaokutisha

Hii inarejerea kwa walewale wadaiwa. Watawatisha Wakaldayo kwa kuwashambulia kulipa kisasi kwa deni lisilo la haki kwamba walikuwa wamelazimishwa kuwa nalo.

inuka juu

"kuongezeka zaidi" au "kuwa na nguvu zaidi"

iliyotekwa nyara

kuibiwa au kuchukuliwa kwa nguvu.

Habakkuk 2:9

Taarifa kwa Ujumla:

Yahwe anaendelea kumjibu Habakuki. Ingawa narejerea kwa Wakaldayo kama kwa mtu mmoja.

ambaye gawa mapato mabaya nyumbani mwake

"ambaye anafanya kazi kupata faida isiyo ya uaminifu kwaajili ya familia yake"

weka kiota chake juu

"jenga nyumba yake mbali na matatizo"

mkono wa mwovu

NI: "mkono wa mwovu" Kutenda "uovu" kama mtu au "watu waovu"

Umebuni aibu kwaajili ya nyumba yako kwa kuondoa watu wengi

"Kwasababu umeondoa watu wengi, familia yako itakuwa inateseka kwa aibu"

Wewe

Umoja

Kuondoa

Kuharibu

umetenda dhambi kinyume chako wewe mwenyewe

"umiza wewe mwenyewe"

mawe ... pao la mbao

"mawe" na "pao la mabo" kuwakilisha watu walioumizwa katika jengo la nyumba, ambao kinyume chake wanawakilishwa watu walioharibiwa na Wakaldayo.

paza sauti

fanya mashitaka kwa Mungu kinyume wajenzi wa nyumba

wajibu

kubaliana na mashitaka

Habakkuk 2:12

Taarifa kwa Ujumla

Yahwe anaendelea kumjibu Habakuki. Ingwa anarejerea kwao Wakaldayo kama kwa mtu mmoja.

Ole kwa yule ambaye anajenga jiji kwa damu, na ambaye anaimarisha mji katika uovu

Kauli hizi mbili zinasema kitu kile kile katika njia mbili tofauti. Tafsiri zinazoingiliana: "Onyo kwa Wakaldayo ambao wanajenga miji yao kwa vile walivyoiba kutoka kwa watu ambao wamewaua"

pamoja na damu

kwa kuua watu. Tafsiri inayopokezana: "yule anayeua watu na kuiba mali zao ili kwamba ajenge mji."

Anayeanzisha mji katika uovu

"Yule anayeanza mji kupitia tabia mbovu." Wakaldayo wanajenga miji yao wakitumia mali zilizoibwa kutoka kwa watu waliowaua.

Hii haikutoka kwa Yahwe wa majeshi kwamba watu wafanye kazi kwa moto na mataifa yote mengine yachoke bila kitu?

Mungu amesababisha uharibifu wa kile watu walichojenga. Ilisemwa katika njia mbili tofauti ili kufanya iwe wazi zaidi. Tafsiri inayobadilishana: "Yahwe ndiye yule anayesababisha watu wanaofanya kazi ngumu ya kujenga kuharibiwa kwa moto na matokeo ni hakuna."

Habakkuk 2:15

Taarifa kwa Ujumla:

Yahwe anaendelea kumjibu cssdved Habakuki. Yeye anarejerea kwa Wakaldayo ingawa kama wako mtu mmoja.

ongeza sumu yako

"ongeza sumu yako kwenye kinywaji"

Utavimbiwa na aibu zaidi kuliko utukufu

"Kama unatafuta utukufu mkuu, Mungu ataleta juu yake aibu kuu"

Wewe

umoja

Kuinywa

Kunywa kikombe cha sumu

Kikome cha mkono wa kuume wa Yahwe kitakugeukia wewe

"Kama Yahwe amehukumu mataifa mengine na uweza wake wote, hivyo atakuhukumu wewe na uweza wake wote"

Kikombe

Divai iliyotiwa sumu

Mkono wa kuume

mkono wa nguvu zaidi

utakuja katika hali yake kukugeukia wewe

"utakuja kwako kama ulivyofanya kwa wengine"

Aibu itafunika heshima yako

"kila mmoja ataona aibu yako na hakuna atakayeona heshima yako"

Habakkuk 2:17

Taarifa ya Ujumla:

Mungu anaendelea kuongea jinsi yaye atakavyo wahukumu Wakaldayo

Kuharibiwa kwa wanyama kutakutisha wewe

"vifo vya wanyama vitakufanya wewe uogope"

Habakkuk 2:18

wewe

neno "wewe" linarejerea kwa Wakaldayo.

subu sanamu

Hii ni kazi ya kuunda sanamu kwa kimiminiko cha chuma katika kitu kilichochongoka katika muundo unaohitajika. chuma kitachukua mwonekano uliosubu na gumu kama picha au sanamu.

metali

Hili ni neno chuma ikiwa katika hali ya majimaji.

mwalimu wa waongo

Kauli hii inarejerea kwa yule aliyechonga au kusubu sanamu. Kwa kutengeneza mungu wa uongo, yeye anafundisha uongo.

Habakkuk 3

Habakkuk 3:1

Nimesikia taarifa zako

Hii inaweza kumaanisha 1) "nimesikia watu wanasema kuhusu kile ulichofanya" au 2) "nilisikia kile ulichosema."

fufua kazi yako

"huisha tena kazi yako" au "fanya tena ulichofanya"

fanya ijulikane

"fanya kazi yako ijulikane"

Habakkuk 3:4

Taarifa kwa ujumla

Habakuki anaendelea kufafanua maono yake ya Yahwe.

miali

Hii ni mistari inayotoka kwenye kitovu cha kitu cha mwanga ambayo inatokea kwenye mwanga asili kama vile jua.

yeye ... yeye ... yeye

Yahwe

Habakkuk 3:6

Taarifa kwa ujumla:

Habakuki anaendelea kufafanua maono yake ya Yahwe.

alipima dunia

Hii inaweza kumaanisha 1) yeye kaikagua kama ambavyo mwenye mamlaka angelifanya kabla hajagawa maeneo kwa watawala au 2) ameitikisa

milima ya milele ... vilima visivyo na mwisho

"milima ambayo imekuwepo tangu mwanzo wa wakati ... vilima ambavyo vitakuwapo mpaka mwisho wa wakati. kama lugha yako haina maneno tofauti kwa "vilima" na "vilima" au kwa "milele" na "usiomwisho" unaweza ukayaweka pamoja kama ilivyo kwenye ULB.

inama chini

katika kumwabudu Mungu. "walilala chini ya ardhi"

Habakkuk 3:7

Taarifa kwa Ujumla:

Habakuki anaendelea kufafanua maono yake ya Yahwe.

mahema ya wakushi katika mateso, na kitambaa cha mahema ... ya Midiani yanatetemeka.

Watu wa Midiani na Wakushi wanao tetemeka na tikisika kwa woga wanafanana na hema ya nguo ambavyo inaenda wakati upepo unavuma.

wakushi

Hii inaweza kuwa 1) jina la kikundi cha watu wasiojulikana vinginevyo au 2) Kushi ile ile.

Yahwe alikuwa na hasira pale mtoni? Ghadhabu yako ilikuwa kinyume na mtoni, au chuki yako kinyume na bahari ... magari ya ushindi?

kama lugha yako haina maneno yakutenganisha "hasira" na "ghadhabu" na "chuki" unaweza ukaunganisha misitari: "Yahwe alikuwa na hasira na mito? Chuki yako ilikuwa kinyume na bahari ... magari ya ushindi?" NI: "Yahwe hakuwa na hasira na mito, wala Chuki yako haikuwa kinyume na bahari ... magari ya ushindi."

fimbo yako juu ya farasi na magari ya ushindi

Kama askari aliongoza farasi au gari katika vita, Yahwe alikuja kuokoa watu wa Isrseli.

Habakkuk 3:9

Sela

Neno hili linamaanisha "simama na akisi" au "inua juu, inua"

Milima ilikuona wewe na ikatikisika kwa maumivu

Kama Mungu aliigawa nchi, milima ilihama, kama vile ingeliona matendo ya Mungu na kudhihirisha kwa kugeuka kutoka pale ilipogawanyika nchi.

kina cha bahari kilipaza sauti

sauti ya mawimbi makubwa ya bahari

iliinua juu mawimbi yake

kiwango cha maji kinaiinuka

Habakkuk 3:11

Taarifa kwa Ujumla:

Habakuki anaendelea kufafanua maono yake ya Yahwe.

katika mwanga wa mshale wako

kwasababu ya mwanga (mng'ao)wa mshale wa Yahwe ulikuwa unang'aa sana.

Umetembea katika ardhi kwa uchungu. Katika hasira umepukutisha mataifa.

Sentensi hizi mbili zinashiriki maana sawa. Kwa pamoja zinarejerea Yahwe anahukumu mataifa kwaajili ya uovu wake.

uchungu

hasira kwa kitu furani ambacho ni kosa

Habakkuk 3:13

Taarifa kwa Ujumla:

Habakuki anamfafanua Yahwe.

mteule wako

Hii inaweza kumaanisha pia "Masihi wako" lakini mrejeo ni wazi "kwa watu wako" hivyo tumia nomino ya kawada hapa, siyo kama jina halisi.

Unapondaponda kichwa cha nyumba ya mwovu

"Unaharibu kabisa kiongozi wa watu waovu"

Habakkuk 3:14

Taarifa Kwa Ujumla:

Habakuki anamfafanua Yahwe kuwaharibu Wakaldayo.

Wanakuja sawa na tufani

Nguvu na uharaka wa Wakaldayo walivyowashambulia Israeli unalinganishwa na ujio wa ghafla wa tufani.

Kuchekelea/cheka

"kujigamba"

teketeza maskini katika mahali palipo fichika

tafuta watu maskini ambao wamejificha na huwaua na kuchukua mali zao zote

teketeza/meza

hula kila kitu kwa haraka

Habakkuk 3:16

Taarifa kwa Ujumla:

Habakuki anafafanua hofu yake anapofikiri kuhusu Yahwe angewapa adhabu Wakaldayo.

ndani yangu kulitetemeka! midomo yangu ilitetema ... uozo huja kwenye mifupa yangu ... chini yangu mwenyewe natetemeka.

haya yanarejerea hofu iliyosababishwa na kufikiri kuhusu matukio yajayo. Habakuki anatumia baadhi ya sehemu za mwili wake kudhihirisha kwamba kila kiungo chake kinahofu.

oza

chakaa

Habakkuk 3:17

mti mtini ... mizabibu ... mzaituni ... mashamba ... kundi ... ng'ombe

Hakuna chakula. Karibu aina zote za vyanzo vya chakula vinavyo patikana katika nchi ya Israeli.

Habakkuk 3:18

Taarifa kwa ujumla:

Habakuki anamtukuza Yahwe.

furahia ... uwe na furaha

Maneno yote yanamaanisha "uwe na shangwe," lakini kama lugha yako ina neno maalumu kwaajili ya kufurahia baada ya kushinda vita, litumie hilo "shangilia sana" hapa

hufanya miguu yangu kama kulungu; huniongoza mahali pangu pa juu

Miguu kama ya kulungu ingempa Habakuki uwezo kupanda ulioinuka mwamba majabari. Maneno "mahali pa juu" linarejerea mahali pa nje kufikiwa na hatari. Yeye anasema Mungu anampa yeye uwezo wa kutafuta mahali pa usalama.

Zephaniah 1

Zephaniah 1:1

neno la Yahweh lililokuja

"neno ambalo Yahweh Mungu alilisema"

Nitaangamiza kabisa kila kitu kutoka usoni mwa dunia...Nitamkata mwanadamu kutoka katika uso wa dunia

Haya ni makusudi kwa ukuzaji wa Yahweh kueleza hasira yake kwa dhambi za watu.

Kukata

Kuangamiza limezungumzwa kama kilikuwa kikikatwa kitu fulani kutoka mahali pake.

Zephaniah 1:4

Milcom

"Milcom" labda ni jina lingine kwa sanamu "Molech."

Zephaniah 1:7

Yahweh ameandaa sadaka na amewatenga wageni wake

Lugha hii inaonyesha mwisho wa mpango wa Mungu na jinsi anavyowatumia adui za watu wake kukamilisha makusudi yake.

Katika siku ilie

"Katika siku ya Yahweh"

kila mmoja amevaa mavazi ya kigeni

maneno haya yanaonyesha kwamba Waisraeli walivaa nguo sawa na za wageni kuonyesha huruma kwa mila zao na kwa ibada zao kwa miungu ya kigeni.

Katika siku ile

"Katika siku ya Yahweh"

Zephaniah 1:10

Tamko la Yahweh

"Yahweh ametamka nini" au "Nini Yahweh amesema kwa makini"

Lango la Samaki

Lango la Samaki lilikuwa mojawapo la malango ukutani mwa mji.

Kuomboleza kutoka kwenye Wilaya ya Pili

"Kuomboleza kwa sauti kubwa kutoka kwenye Wilaya ya Pili." Wilaya Pili ilikuwa karibu sehemu ya Yerusalemu.

kutoka milimani

Hii inahusu milima inayozunguka Yesusalemu. "kutoka milima inayozunguka Yerusamu."

kwa wafanyabiashara wote watakuwa wameharibiwa; wale wote wanaopima fedha watakuwa wamekatiliwa mbali

"kwa wale ambao hununua na kuuza bidhaa, wafanyabiashara, watakuwa wameuwawa."

Zephaniah 1:12

Nitaichungua Yerusalemu kwa taa

Hakuna hata mmoja atakayeweza kujificha kutoka kwa Mungu.

makazi kwenye mvinyo yao

Watajisikia salama kutoka kwenye shida

na kusema moyoni mwao

Watasema kwa uhakika

Zephaniah 1:14

karibu, karibu na inaharakisha haraka

Marudio ya neno "karibu," pamoja na maneno "inaharakisha haraka" inasisitiza kwamba siku wakati Yahweh anahukumu watu haraka itatokea. "karibu na itakuwa hapa haraka."

Siku hiyo itakuwa siku ya ghadhabu ... buruji

Kauli hii ni kusisitiza jinsi hukumu ya Mungu itakavyokuwa ya kutisha. Namba nyingi za hotuba zinaongezeka na kuonyesha uharibifu wa asili ya hukumu hii ya mwisho ya Mungu. Inajenga mkazo.

siku ya shida na uchungu

Neno "shida" na "uchungu" inamaanisha kuhusu kitu kilicho sawa na kusisitiza ukali wa shida za watu.

siku ya dhoruba na uharibifu

Hapa neno "dhoruba" inahusu hukunu ya Mungu. Neno "uharibifu" inaelezea madhara ya hukumu ile. "siku ya inayoharibiwa na dhoriuba" au siku ya kuharibiwa na hukumu." (na

siku ya giza na viza

Neno "giza" na "viza" linashiriki maana sawa na kusisitiza kiwango giza. Maneno yote yanalejea kwenye wakati wa maafa au hukumu ya Mungu. "Siku ambayo imejaa giza." au "siku ya hukumu ya kutisha."

siku ya mawingu na giza nene

maneno haya yanamaanisha kitu kilicho sawa kama, na linaongezezea wazo la maneno yaliyotangulia. kama maneno haya, yote "mawingu" na "giza nene" inarejea kwenye hukumu ya Mungu. "siku iliyojaa dhoruba lenye mawiingu yenye giza." (na

siku ya panda na kengele

Maneno "panda" na "kengele" kimsingi yanamaananisha kitu kilicho sawa hapa. Yote yanamaanisha kuita askari kujiandaa kwa vita. "siku wakati watu watakapotoa sauti ya kengele ya vita."

mada ni miji na buruji ndefu

Misemo hii miwili yote inarejea kwenye nguvu ya kijeshi inayoshikilia. " mada ni miji mizuri."

Zephaniah 1:17

tembea kama wanaume vipofu ... waliomwagwa kama vumbi ... sehemu zao za ndani kama samadi

misemo hii mitatu inaashiria ulinganifu kuonyesha nini vilicho nacho kikawaida.

moto wa wivu wake

Hii inahusu nguvu ya hasira ya Yahweh.

Zephaniah 2

Zephaniah 2:1

Mkutano wa hadhara ninyi wenyewe pamoja na kusanyikeni

Misemo hii miwili ina maana ya kitu sawa. Pamoja vinaimarisha amri kwa watu kukusanyika pamoja kwa ajili ya kutubu dhambi zao. "kusanyikeni ninyi wenyewe pamoja."

taifa lisilokuwa na aibu

Taifa halina pole kwa dhambi zake.

siku hiyo inapita kama makapi

Makapi hayamaanishi sehemu ya kilichopandwa kuwa kilitupwa mbali na hivyo siku hii itapita haraka.

kabla hasira kali ya ghadhabu ya Yahweh kuja juu yako, kabla ya siku ya ghadhabu ya Yahweh kuja juu yako

Mtume anarudia msemo uleule karibu hasa ili kusisitiza jinsi hukumu ya Yahweh ilivyo ya kutisha itakavyokuwa na uharaka ambao watu lazima watubu.

Ghadhabu ya Yahweh

Hili linasimama kwa dhamira Mungu kuhukumu.

Zephaniah 2:4

Watamtoa nje Ashdod wakati wa mchana, na watamng'oa Ekron!

Watu kwa haraka watakuwepo na kabisa wataondolewa kutoka miji hii.

Mpaka hakuna mwenyeji atakayebakia

"Mpaka hakuna hata mmoja atakayekuwa pale"

Zephaniah 2:6

Hivyo pwani itakuwa ... kalamu za kondoo

Sehemu ya msitari huu maana yake haiko wazi na imetafsiriwa kwa njia tofauti kwa matoleo ya kisasa

Kalamu za kondoo

Kalamu ya kondoo ni sehemu ndogo iliyozungushiwa uzio kuweka kondoo pamoja.

kulala chini

inamaanisha kulala kitandani

Zephaniah 2:8

tamko la Yahweh wa majeshi

"Yahweh wa majeshi ametamka nini" au "Yahweh wa majeshi amesema ameweka nini"

Zephaniah 2:10

fahari, kiburi, kiburi kilichojaa

Swala, "fahari" na "kiburi kilichojaa" linarejea kwa mtu anayefikiria kwa juu zaidi yeye mwenyewe, na hasa, anafikiria kwamba yeye ni bora kuliko watu wengine.

dharau, kejeli, mzaha katika

Swala hili "dharau," "kejeli" na "mzaha katika" yote yanahusu kumfanya mtu kuwa na furaha, hasa katika njia ya kikatili.

hofu, woga, hofu ya Yahweh

Mapendekezo ya tafsiri

mungu wa uongo, mungu wa kigeni, mungu, mungu wa kike

Mungu wa uongo ni kitu ambacho watu hukiabudu badala ya Mungu mmoja wa kweli* Suala hili "mungu wa kike" linahusika hasa kwa mungu wa uongo wa jinsia ya kike

nchi, kidunia

Suala hili "nchi" linahusika na ulimwengu ambao mwanadamu alikuwa akiishi juu yake, pamoja na wanateolojia wote wa uhai.

Mapendekezo ya tafsiri

ibada

"Kuabudu" maana yake ni heshima, sifa na kumtii mtu fulani, hasa Mungu.

Mapendekezo ya tafsiri

Suala hili "ibada" linaweza kutafsiriwa kama "kuinama chini kwa" au "heshima na kutumika" au "heshima na kutii."

Zephaniah 2:12

juu ya nguzo zake

Wakati majengo yalipoharibiwa na kuanguka chini, nguzo zilitumika kwa kupamba na msaada mara kwa mara ulibakia umesimama.

mihimili

mihimili ni mirefu na vipande vinene vya mti ambavyo vilitumika kuweka jengo imara.

Zephaniah 2:15

kuzomea na kuitingisha ngumi yake

Kuzomea ni sauti ya ukali. Maneno haya yanaonyesha hasira iliyokithiri ya watu walioelekea Ninawi.

Zephaniah 3

Zephaniah 3:1

Hakuisikiliza sauti ya Mungu

Watu wa Yerusalemu hawakutii ambacho Mungu alikuwa nacho kwa mitume wake chakuwafundisha.

na hawatamkaribia Mungu wao

Watu hawakutamani kumwabudu na kumtii Mungu.

Zephaniah 3:3

Wakuu wao ni simba waungurumao katikati yao

"Viongozi wa Yerusalemu ni wenye vurugu"

Majaji wao ni mbwa mwitu wa jioni wasiobakiza chochote ambacho kitakuwa kimetafunwa mpaka asubuhi

"Majaji wao ni watu waovu ambao huchukua vitu ambavyo ni mali za wengine." Hii pia ni mfano.

Manabii wao ni wadhulumaji na wanaume wahaini."

"Manabii wao siowatii na wanaume wasio waaminifu."

Zephaniah 3:5

Haitafichika nuruni

"haki yake imeonyeshwa wazi kwa wote."

Zephaniah 3:6

Nimeifanya mitaa yao magofu, hivyo hakuna atakayepita juu yao. Miji yao imeharibiwa hivyo hakuna mwanaume atakayekaa humo

Yahweh anaelezea wazo lililo sawa kwa njia mbili tofauti ili kusisitiza ukamilifu wa uharibifu wa miji.

Zephaniah 3:8

Tamko la Yahweh

Hii inamaanisha Yahweh amesema kwa makini.

Inuka kwa waathirika

"Inuka kuangamiza waathirika"

kuyakusanya mataifa, kuzikusanya falme

Maneno haya mawili yanamaanisha kitu sawa na kusisitiza kwamba Yahweh atayahukumu mataifa yote.

hasira yangu, ghadhabu yangu kali yote

Maneno "hasira" na "ghadhabu kali" kimsingi ina maana sawa na inasisitiza kiwango cha hasira ya Yahweh. "hasira yangu kali."

hivyo nchi yote itakuwa imemezwa kwa moto wa hasira yangu

Maneno haya yanaweza kuelezewa kwa mfumo wa kitendo. "kwa hiyo moto wa hasira yangu utameza nchi yote."

kuteketezwa kwa moto wa hasira yangu

Hasira hapa imesemwa kama kutakuwa na moto ambao utateketeza kitu fulani.

Zephaniah 3:9

Nitawapa midomo safi watu

Hii ni njia nyingine ya kusema kwamba Mungu atasababisha watu wake kusema ambacho ni haki.

nitumikieni mimi mkisimama bega kwa bega

Watu wataunganishwa kwa hamu zao kumtumikia Mungu, kama watu wameunganishwa kimwili watakaposimama pamoja kwa mabega yao yakigusana kila mmoja.

Zephaniah 3:12

hakuna ulimi wa udanganyifu utakaoonekana mdomoni mwao

"hakuna hata mmoja atakayeonekana na ulimi wa udanganyifu mdomoni mwake" au "hawatasema vitu vya udanganyifu."

watafunga na kulala chini

Yahweh husema kwa watu wa israeli kama wao ni kundi la kondoo wanaofunga na kupumzika kwa usalama.

Zephaniah 3:14

binti Sayuni

"Hii inamaanisha watu wote wa Yerusalemu.

Usiiache mikono yako ilegee

Hii inamaanisha usijisikie dhaifu au mnyonge unavyokuwa kama mikono yako itakuwa dhaifu kimwili.

Zephaniah 3:17

hodari, nguvu

Masuala haya "hodari" na "nguvu" hurejea kuwa na nguvu kubwa au uwezo. . Mara nyingi neno "nguvu" ni neno lingine kwa "nguvu."Tunapozungumza kuhusu Mungu, inaweza kumaanisha "Uwezo." . Maneno, "wanaume wenye nguvu" mara kwa mara inahusu wanaume ambao ni wajasiri na wanaoshinda vita. Bendi ya Daudi ya wanaume waaminifu iliyomsaidia kumlinda na kumtetea mara kwa mara ilikuwa inaitwa "wanaume hodari."

Zephaniah 3:19

Nitamwokoa kilema na kumkusanya aliyefukuzwa

Hii inaonekana kurejea kwa kilema na kondoo aliyefukuzwa, ambaye anatumika kwa picha ya Waisraeli walioteseka utumwani.

Nitawatengeneza wao kama sifa

Wazo zima hapa ni, "Nitawatengeneza wao kuwa vitu vya kusifiwa," hiyo ni, "Nitawatengeneza wao kusifiwa kwa wengine."

Katika wakati ule nitakuongoza; katika wakati ule nitakukusanya pamoja

Misitari hii miwili kimsingi ina maana ya kitu kilichosawa na kuashiria kwamba Yahweh atawaleta nyuma watu uhamishoni katika nchi yao. "Katika wakati ule nitakukusanya pamoja na kukuongoza nyumbani."

Haggai 1

Haggai 1:1

mwaka wa pili wa mfalme Dario

"mwaka wa pili wa utawala wa mfalme Dario"

Dario...Haghai...Zeubabeli...Shealtieli...Yehozadaki

Haya yote ni majina ya wanaume.

katika mwezi wa sita, siku ya kwanza ya mwezi

"katika siku ya kwana ya mwezi wa sita." Huu ni mwezi wa sita wa karenda ya kiebrania. Siku ya kwanza ni karibu na katikati ya mwezi wa nanekwa karenda ya kimagharibi.

ulikuja kupitia mkono wa Haghai

Haghai alikuwa mjumbe.

Haggai 1:3

kwa mkono wa Haghai

"Ulikuja kupitia maneno" (au 'mdomo') wa Haghai

ni wakati wenu wa kukaa kwenye nyumba zenu zilizokamilika?

Tazama UDB

wakati nyumba hii inaharibika

Neno "Nyumba" hapa inamaanisha hekalu ya Mungu.

lakini usilewe

Hapa aya hii haimaanishi kuwa kulewa siyo kitu kizuri. Badala yake hakuna mvinyo unaoweza kukidhi kiu ya watu na haitoshi kwa kunywa.

mishahara mnayopata ya fedha mnaweka kwenye mfungo ambao umejaa mashimo

"pesa unayotengeneza kazini haiwezi kukunulia vitu vya kutosha"

Haggai 1:7

leta mbao

Hii inawakilisha sehemu tu ya kile walitaka kujenga katika Hekalu

asema Bwana wa Majeshi

"Haya anayesema Bwana wa Majeshi" au "Ndivyo alivyosema kweli Bwana wa majeshi"

Haggai 1:10

mbingu

"Anga"

kutoa umande

"kutoa mvua"

ukame

ukame ambao utazuia au kukwamisha mimea na kukausha maji yote ambayo yanahitakija kwa ajili ya wanyam na watu walio katika eneo hilo.

juu ya mzabibu mpya na juu ya mafuta

mvinyo unafawikilisha zabibu na mafuta yanawakilisha mzeituni

kazi za mikono yako

"kazi zako zote ulizofanya kwa bidii!" na UDB

Haggai 1:12

na maneno ya nabii Haghai

"waliposikia maneno ambayo nabii Haghai aliyasema"

uso ya Bwana

"Bwana"

Asema Bwana

"kile Bwana amesema" au "kile Bwana kweli alisema"

Haggai 1:14

alitibua roho

Hii inamaanisha kuhamasisha au kushawishi.

mabaki

Neno "Mabaki"linatokana na watu waliobaki hai wakiwa wanatoka utumwani Babeli na walianza kuujenga Yerusalemu tena.

katika siku ya ishirini na nne Mwezi wa sita

siku ya nne ya mwezi wa sita - Hii ni siku 23 tu baada ya kupata maono. Huu ni mwezi wa sita kwa kalenda ya kiebrania. Siku ya ishirini na nne ni karibu na katikati ya mwezi wa tisa kwa kalenda za kimagharibi.

mwaka wa pili wa Mfalme Dario.

"mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario"

Haggai 2

Haggai 2:1

Katika Mwezi wa saba siku ya ishirini na moja ya mwezi

siku ya kwanza ya mwezi- Huu ni mwezi wa saba wa kalenda ya Kiebrania. Siku ya ishirini na moja ni karibu na katikati ya mwezi wa kumi wa kalenda ya kimagharibi.

lilikuja kwa mkono wa Nabii Hagai

tazama

Haghai... Zerubabeli...Sheltiel...Yehozadaki

tazama

Haggai 2:3

si chochote machoni penu?

"Ni lazima uwaze kwa hakika na si lazima hata kidogo"

Sasa, muwe hodari

"Kutoka sasa na kuendelea muwe hodari"

Haggai 2:6

nitatikisa mbingu na dunia

ni usumbufu mkubwa sana

Haggai 2:8

Dhahabu na fedha ni vyangu

Maneno Fedha na dhahabu" yanamaanisha hazina zinazoletwa hekaluni.

Haggai 2:10

Katika siku ya ishirini na nne mwezi wa tisa

siku ya nne ya mwezi wa tisa - Huu ni mwezi wa tisa wa kalenda ya kiebrania. siku ya ishiri na nne ni karibu na katikati ya mwezi wa kumi na mbili wa kalenda ya magharibi.

mwaka wa pili wa utawala wa Dario

"mwaka wa pili wa utawala wa mfalme Dario

Dario... Haghai

Tazama

Haggai 2:13

pamoja na hawa watu na pamoja na taifa liliko mbele yangu!

"Hii ni kweli na watu wa Israeli!" au "Hii ni kanuni ileile walioishika kweli kwa ajili ya watu wa Israel!"

Haggai 2:15

Kwa hiyo, fikiri kutoka siku hii ya leo na kuendelea

"Kumbuka ilikuwa inafananaje"

vipimo ishirini vya nafaka

"Vipimo" ni kiasi kisichojulikana

vipimo hamsini vya divai

"Vipimo" ni kiasi kisichojulikana

Niliwataabisha ninyi na kazi za mikono yenu

"Niliilani kazi yenuna mazao yenu yote".

Haggai 2:18

siku ya ishirini na nne katika mwezi mwezi wa tisa

siku ya nne ya mwezi wa tisa * _ tazama ulivyoitafsiri hii.

je, bado kuna mbegu katika ghala?

Jibu lililotarajiwa ni "Hapana" hili swali lilitumika kuonyesha wasomaji kile walikuwa wanakijua.

mti wa mtini, komamanga, na mti wa mzeituni

Haya ni matunda yaliyokuwa yanalimwa katika ardhi hiyo.

Haggai 2:20

Haghai... Zerubabel

Haya ni majina ya wanaume.

siku ya ishirini na nne ya mwezi

siku ya nee ya mwezi "Katika siku ya ishirini na nne mwezi wa tisa

nitatikisa mbingu na nchi

Bwana atasabisha usumbufu katika nchi yao.

mbingu na nchi

"ulimwengu wote"

nitakiangusha kiti cha wafalme

Serikali zitaangushwa kwenye machafuko.

Kiti cha kifalme

"serikali zilizoongozwa na wafalme"

upanga wa ndugu

"Upanga wa askari mwenzake"

Zechariah 1

Zechariah 1:1

Katika mwezi wa nane

Huu ni mwezi wa nane katika kalenda ya Kiyahudi. Katika kalenda ya sasa ni mwishoni mwa Octoba na mwanzoni mwa Novemba.

mwaka wa pili wa kumiliki kwake Dario

"mwaka wa pili tangu Dario alipokuwa mfalme"

Neno la Yahwe lilikuja

"Yahwe alinena neno lake"

Berekia...Ido

Haya ni majina ya wanaume.

Yahwe alikuwa na hasira sana juu ya baba zenu

"Kuwakasirikia sana babu zenu"

Nirudieni

Neno "rudi" inamaanisha mabadiliko. Yahwe anawaambia watu wa Israeli kubadilika kutoka kutokumtii na kumtii.

asema Yahwe wa majeshi

Kifungu hiki mara kwa mara kitafasiriwa kama "asema Yahwe" katika UDB. Na kirai hiki kimetumika sana katika kitatu cha Zakaria.

Nitawarudia ninyi

Kwa kusema atawarudia watu wa Israeli, Yahwe anasema watakuwa na mambo mema yakitokea kwa sababu atakuwa akiwasaidia.

Zechariah 1:4

walilia

"kupiga kelele"

Kugeuka kutoka

"kubadilika"

Lakini hawakuweza kusikia wala kunijari

Vifungu hivi vyote vinamaanisha watu wa Israeli wasingeweza kutii maagizo ya Yahwe.

asema Yahwe

Kifungu hiki mara kwa mara kitafasiriwa kama "asema Yahwe" katika UDB. Na kirai hiki kimetumika sana katika kitabu cha Zakaria.

Wako wapi baba zenu? Na manabii, je wapo hapa daima?

Maswali haya yote yameulizwa kuonesha kwamba kwa kweli watu wanakufa.

Lakini maneno yangu na maagizo niliyowaamru watumishi wangu manabii, je hayakuwapata baba zenu?

Maswali haya yametumika kuonesha watu wa Israeli kwamba kila jambo ambalo Bwana alikuwa amewaambia manabii wake kuwaonya babu zao, yalikuwa yametimia.

Maneno yangu na amri zangu

Hii yote inaonesha Mungu aliyokuwa ameyasema kwa manabii.

kuwapata baba zenu

Yahwe anazungumzia unabii wake kama vile unawakimbilia babu zao ili uwapite. Neno "kupata" lamaanisha kuwapita

matendo na njia zetu

"mwenendo na matendo yetu"

Zechariah 1:7

Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kumi na moja, ndiyo mwezi wa Shebati,

siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kumi na moja, ndiyo mwezi wa Shebati - "Shebat" ni mwezi wa kumi na moja katika kalenda ya Kiebrania. Siku ya ishirini na nne ni sawa na karibu katikati ya mwezi wa pili katika kalenda ya sasa.

Neno la Yahwe lilikuja

Yahwe alisema neno lake

Berekia... Ido

Haya ni majina ya wanaume.

miti ya mihadasi

ni aina ya miti midogo yenye maua yenye rangi.

Zechariah 1:10

Hawa ni wale... Walijibu

Maneno "hawa" na "wale" inamaanisha farasi kati ya miti ya mihadasi

kuzunguka duniani

Maana yaweza kuwa: 1) "kuiangalia dunia yote" au 2) "kutembea duniani mwote"

kati ya miti ya mihadasi

ni aina ya miti midogo yenye maua yenye rangi

dunia yote imetulia na kustarehe

"watu wote duniani walikuwa na amani"

imekaa na kuwa na amani

Vifungu vyote vinamaanisha kuweza kutulia pasipo na cha kuogopa.

Zechariah 1:12

imeteswa na kudhurumiwa

Maana pendekezwa 1) "umekuwa na hasira juu(UDB) au 2) "imekuwa ikitendewa bila heshima"

nena nami, kwa maneno mazuru, maneno ya faraja

Vifungu hivi vinazungumzia maneno ambayo ni mema na ya faraja.

Zechariah 1:14

Nami nina hasira juu ya mataifa yaliyo na utulivu

Nimekarishwa sana na mataifa yanayofurahia amani na usalama"

Nilikasirika kidogo tu

"Nilikuwa na hasira kidogo tu na watu wa Yuda"

Zechariah 1:16

Nimeirudia Yerusalemu kwa rehema nyingi

Kurudi Yerusalemu inamaanisha kuchukua tena jukumu la kuwaudumia watu wa Israeli kama mfalme kurudi kuwaongoza watu kutoka katika shida.

Nyumba yangu itajengwa ndani yake

"Hii inamaanisha kujengwa tena kwa hekalu katika Yerusalem"

hili ni tamko la Yahwe wa majeshi

Kifungu hiki mara kwa mara kinafasiriwa kama "asema Yahwe." Na kifungu hiki kimetumika mara kwa mara katika kitabu hiki.

Kipimo kitanyoshwa juu ya Yerusalemu

"Yerusalemu itakaguliwa kabla ya kujengwa"

Miji yangu kwa mara nyingine itajawa na uzuri

Yahwe anamaanisha mambo mema atakayoyafanya kwa ajili ya watu wake Israeli kama ambavyo kimiminika kinavyoweza kujaa katika miji na kufurika.

Yahwe ataifariji tena Sayuni

"Yahwe atawatia moyo watu wa Israeli"

Zechariah 1:18

Maelezo ya Jumla:

Zakaria anaendelea kuelezea ono lake

Niliinua macho yangu

Kifungu hiki kinamaanisha kuelekeza kichwa chako katika kutazama

pembe ziliyoitawanya Yuda

Hii inawakilisha majeshi yaliyowashambulia watu wa Israeli.

Zechariah 1:20

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anaendelea kuelezea maono ya Zakaria kwa ajili yake.

Wafua chuma

Watu wanaofanya kazi ya kutengeneza vitu kutokana na chuma. Wanatumika kumaanisha upanga wa jeshi.

Pembe zilizomsambaratisha Yuda

Hawa ni majeshi yaliyoishambulia Yuda

Hakuna mtu angeinua kichwa chake

Hii inamaanisha mtu anayeogopa kutazama kitu kinachomwogopesha.

Kuwaondoa

"kuondoa hayo mataifa"

kuzitupa pembe chini

"kuwashinda maadui"

kuinua pembe yoyote

hii inamaana ya kupuliza pembe ili kuliamuru jeshi.

Zechariah 2

Zechariah 2:1

Maelezo ya Jumla:

Zakaria anaendelea kuelezea maono yake.

Niliinua macho yangu

"Nilitazama juu"

kipimo cha kupimia

kamba yenye urefu fulani inayotumika kwa kupima vitu vikubwa.

Hivyo aliniambia

"Hivyo mtu mwenye kamba ya kupimia aliniambia"

Zechariah 2:3

malaika mwingine akaenda kukutana naye

Huyu ni malaika mwingine ambaye hajawai kutokea hapo mwanzo, na hivyo anatambulishwa kama mshiriki mwingine.

Malaika wa pili akamwambia, "Nenda uongee na mtu yule

Malaika mwingine alimwambia malaika aliyekuwa ameongea na Zakaria, "Nenda haraka uongee na mtu mwenye kipimo"

Yerusalemu inakaa katika nchi wazi

Kifungu hiki kinamaanisha kwamba Yerusalemu haitazungukwa na kuta.

kuwa kwake ukuta wa moto kumzunguka

Yahwe anasema atailinda Yerusalemu na kulinganisha ulinzi wake na ukuta wa moto.

Hili ni tamko la Yahwe

Kifungu hiki wakati mwingine kinatafasiriwa kama asema Yahwe.

Zechariah 2:6

Kimbieni! kimbieni!

Maneno haya yamerudiwa na yanaonesha umuhimu kwa ujumbe unaofata. Umetumika mara mbili kwa sababu ujumbe ni mhimu sana.

nchi ya kaskazini

Inamaanisha Babeli

nimewatawanya kama pepo nne za anga

Hii inamaanisha watu wa Israeli wako mbali mmoja kwa mwingine. Pepo nne zinamaanisha sehemu mbalimbali za dunia.

binti Babeli

Hii inamaanisha mji mkuu wa Babeli.

Zechariah 2:8

Maelezo ya Jumla:

Zakaria anasema jinsi Yahwe anavyomtuma kuwahukumu mataifa walioiteka Yerusalemu.

Kuwateka ninyi

"kuiba vitu kutoka Yerusalemu baada ya kuwa imeshambuliwa"

maana kila akugusaye

"Kugusa" inamaanisha kudhuru

mboni ya jicho la Mungu

mboni ya jicho inamaanisha sehemu nyeusi katika jicho inayomwezesha mtu kuona. Hii ni sehemu muhimu sana katika mwili wa mtu. Hii inaonesha kwamba Yerusalemu ni ya muhimu sana kwa Mungu na ni kitu ambacho Mungu atakilinda.

tikisa mkono wangu juu yao

hii ni ishara inayotumika kuonesha Mungu amechagua Kuharibu jambo fulani.

na watakuwa mateka

Miji yao imeharibiwa tiyari na imeachwa wazi kwa watu kuiba chochote watakacho.

Zechariah 2:10

binti Sayuni

Hili ni jina lingine kwa Yerusalemu linalorejerea kwa mji kama binti wa mji wa Sayuni ya mbinguni.

kupiga kambi

kuweka mahema na kuyatumia

Hili ni tamko la Yahwe

Kifungu hiki wakati mwingine kinatafasiriwa kama asema Yahwe

mataifa watajikusanya kwa Yahwe

"mataifa yatamtii Yahwe"

katika siku hiyo

"kwa wakati ule"

Zechariah 2:12

Yahwe atamiliki... katika nchi takatifu

"Yahwe ataifanya Yuda mali yake ya nchi takatifu"

miili yote

Yahwe anarejerea kwa viumbe hai wote kwa kuwaita miili. Mwili ni kitu walichonacho viumbe wote.

maana ameinuka kutoka mahali patakatifu pake

Hii inamaanisha Yahwe kusababishwa kuchukua hatua juu ya nchi.

Zechariah 3

Zechariah 3:1

Maelezo ya Jumla:

Yahwe anamwonesha ono Zakaria

Je! hiki si kinga kilichotolewa motoni?

"Yoshua ni kama ukuni uliotolewa motoni"

kinga kilichotolewa motoni

Kinga ni kipande cha ukuni uwakao kinachotolewa motoni kabla hakijaisha. Hii inamrejerea Yoshua, aliyeokolewa kutoka mateka ya Babeli na kurudi Yerusalemu.

mavazi machafu

katika ono hili mavazi yanatumika kama alama ya kuonesha dhambi.

Zechariah 3:4

kukuvalisha vazi safi

Hapa vazi safi linatoa alama ya utakatifu.

kilemba

kipande cha nguo kinachozungushwa kichwani

Zechariah 3:6

alimwagiza Yoshua kwa dhati

"alimwagiza Yoshua katika hali ya kuzingatia kwa dhati"

takwenda katika njia zangu

Inamaanisha kutembea katika mapenzi yake.

kama mtatunza maagizo yangu

"ikiwa mtakumbuka na kutii maagizo yangu"

linda nyua zangu

"kuwajibika kwa maeneo yake maalumu"

Zechariah 3:8

Maelezo ya Jumla:

Malaika wa Yahwe anaendelea kuengea na Yoshua.

wenzako wanaoishi nawe

"makuhani wengine wanaoishi nawe"

mtumishi wangu tawi

Jina "tawi" linapaswa kutafisiriwa vilevile kama tawi la mti. Inamaana kuwa mtumishi wa Yahwe atakuja kutoka kwa Yahwe kama tawi litokavyo katika mti.

macho saba

Hizi ni pande saba.

chonga

"chora"

andishi

maneno yaliyoandikwa juu ya kitu fulani au kukatwa katika kitu fulani

hili ni tamko la Yahwe wa majeshi

Kifungu hiki mara nyingi hufasiriwa kama "asema Yahwe"

Zechariah 3:10

katika siku hiyo

"katika wakati huo"

hili ni tamko la Yahwe wa majeshi

Kifungu hiki mara nyingi hufasiriwa kama "asema Yahwe"

Zechariah 4

Zechariah 4:1

kuniamsha kama mtu aamshwavyo usingizini

"kunifanya kuwa na hadhari kama mtu aliyeamshwa usingizini"

vinara vya taa

sehemu za taa vinavyowashwa moto

upande wa kushoto

"upande wa kushoto wa bakuri"

Zechariah 4:4

malaika, malaika mkuu

Malaika ni kiumbe wa kiroho aliyeumbwa na Mungu. Malaika wanaishi kwa kumtumikia Mungu kwa kufanya chochote anachowaambia kufanya. Jina "malaika mkuu" linamhusu malaika anayetawala au kuwaongoza malaika wote. . Neno "malaika" kwa kawaida linamaanisha "mjumbe". . Neno "Malaika mkuu" linamaanisha "mjumbe mkuu." Malaika pekee aliyetajwa kama "malaika mkuu" katika Biblia ni Mikaeli. .Katika Biblia, malaika watoa ujumbe kutoka kwa Mungu. Jumbe hizi zinahusisha maelekezo jinsi Mungu alivyotaka watu wafanye.

Pia malaika waliwaambia watu juu ya matukio yaliyokuwa yatendeke au yametendeka. Malaika wanamamlaka ya Mungu kama wawakilishi wake na wakati mwingine walizungumza katika Biblia kama vile Mungu mwenyewe alikuwa akiongea. Njia nyingine malaika wanatumika kwa kuwalinda na kuwatia nguvu watu Kirai maalumu, "malaika wa Yahwe" kina maana zaidi ya Moja: 1) Malaika anayemwakilisha "malaika anayemwakilisha Yahwe" au "mjumbe anayemtumikia Yahwe" 2)Yaweza kumhusu Mungu mwenyewe, anayeonekana kama mwanadamu alipoongea na mtu. Pengine moja kati ya maana hizi yaweza kuelezea matumizi ya "mimi" na malaika kama vile Mungu Mwenyewe alikua akiongea.

bwana(lord), bwana(master), bwana(sir)

Neno "bwana" linamaanisha mtu mwenye umiliki au mamlaka juu ya watu.

Neno hili wakati mwingine linatafasiriwa kama "bwana"(master) linapomweleza Yesu au linapomtaja mtu anayemiliki watumwa. Baadhi ya matoleo ya Kiingereza yanalitafasiri kama bwana(sir) katika mazingira ambapo mtu kwa heshima anamtaja mtu mwenye cheo cha juu.

Jua, maarifa, kutambulisha

"Kujua" inamaanisha kufahamu kitu au kuwa na habari juu ya ukweli. "kujulisha" inamaanisha kusema habari.

Neno "maarifa" lahusu habari anayoijua mtu. Yaweza kujua jambo katika ulimwengu wa roho au mwili. "kujua kuhusu" Mungu yamaanisha kufahamu ukweli kumhusu yeye kwa sababu ya yaliyofunuliwa. "Kujua" Mungu inamaanisha kuwa na uhusiano naye. Hii pia inahusu kuwafahamu watu wengine. Kujua mapenzi ya Mungu yamanisha kufahamu alichokiagiza, au kufahamu anachotaka mtu afanye. "Kujua sheria" kujua alichokiagiza Mungu au kufahamu alichokielekeza Mungu katika sheria ya Musa. Wakati mwingine "maarifa" inatumika kama mbadala wa "hekima," inayohusisha kuishi katika hali inayompendeza Mungu. "Maarifa ya Mungu" wakati mwingine inatumika kama mbadala wa "hofu ya Yahwe."

Zechariah 4:6

Taarifa ya Kuunganisha:

Malaika alinayeongea na Zakaria anaendelea kuelezea ono.

Zerubabeli

Hili ni jina la mwanamme

Siyo kwa nguvu au uwezo

Maana pendekezwa 1) neno "uwezo" na "nguvu" kimsingi lamaanisha jambo lilelile na linasisitiza nguvu ya Zerubabeli, au 2) kwamba neno "uwezo" linamaanisha nguvu za kijeshi na neno "nguvu" linaonesha uwezo wa kimwili wa Zerubabeli.

U nani wewe, mlima mkubwa?

Yahwe anauliza swali hili kwa mlima kuonesha kwamba Roho wa Yahwe, wala siyo mlima ananguvu zaidi ya kumshinda Zerubabeli.

atalishusha jiwe la juu

jiwe la juu ni jiwe la mwisho linalowekwa kitu kinapojengwa.

Zechariah 4:8

Taarifa ya Kuunganisha:

Malaika alinayeongea na Zakaria anaendelea kuelezea ono

Neno la Yahwe lilikuja

"Yahwe alisema neno lake"

Mikono ya Zerubabeli... mikono yake itaimaliza

Zerubabeli anasimamia ujenzi wa hekalu. Kujenga kunatajwa kama "mikono yake" japokuwa yawezekana mikono yake isiweke mawe.

kuweka msingi

Msingi ni chanzo cha jengo na sehemu ya kwanza ya mradi wa ujenzi.

Ni nani aliyezarau... mambo madogo?

Swali hili haliitaji jibu ila linawaambia wasizarau "siku ya mambo madogo."

siku ya mambo madogo

Kifungu hiki ni jina kwa ajili ya wakati ambapo kila siku kazi rahisi zilifanywa. Muda wote wa ujenzi wa jengo unatajwa kama siku moja japokuwa ilichukua miaka kadhaa kukamilika.

Jiwe la kupimia

Jiwe linalounganishwa na kamba. Linatumika kuamua kama kuta za jengo zimenyooka au hapana.

taa saba ni macho ya Yahwe

Hizi taa saba ni alama za macho ya Yahwe.

macho ya Yahwe

Neno "macho" linamtaja Mungu akiona kwa sababu macho hutumika kwa kuona.

Zechariah 4:12

mirija miwili ya dhahabu

"imetengenezwa kwa dhahabu"

Je! wafahamu hivi ni nini?

"Unapaswa kujua hivi ni nini, lakini haujui."

Zechariah 4:14

Hawa ni wana wa mafuta mabichi ya mizeituni

Hii ni njia ya kishairi ya kusema, "watu waliotiwa mafuta"

simama mbele

Taarifa hii inawakilisha wazo la kutumikia.

Zechariah 5

Zechariah 5:1

Kisha niligeuka

Neno "Mimi" linamtaja Zakaria.

kuinua macho yangu

Hii inamaanisha kuangalia juu ya kitu fulani. Anasema "Niliinua macho" kwa sababu hii ni sehemu ya mwili mtu anayotumia kuona.

Tazama

Neno "tazama" linaonesha kwamba Zakaria alishangazwa na alichokiona.

dhiraa

Dhiraha ni sawa na sentimita 46.

Zechariah 5:3

Maelezo ya Jumla:

Malaika anaendelea kuongea na Zakaria.

anakwenda juu ya uso wa

Kifungu hiki kinahusu laana kama wingu linalosambaa kufunika uso wa nchi. Neno "uso" inahusu uso wa nchi kama uso wa mtu juu ya nyuso za kichwa chao.

kutegemea inachosema upande mmoja

"kutegemea na kile ambacho gombo limeandika upande mmoja"

kwa kadili ya maneno yao

Kifungu "maneno yao" kinamaanisha kile kilichosema katika nadhiri zao.

Nitaipeleka

Neno "hiyo" inahusu laana.

hili ni tamko la Yahwe wa majeshi

Kifungu mara nyingi kimefasiriwa kama "asema Yahwe. Kifungu hiki kimetumika mara nyingi katika kitabu cha Zakaria.

nyumba

Hii inamaanisha familia ya mtu na kila anachokimiliki.

wa yule aapaye

"wa yule aapaye"

mbao

mti unaotumika kwa ujenzi.

Zechariah 5:5

Inua macho yako

Kifungu hiki kinamwamru mtu kutazama juu kwa kurejerea macho yake.

Kifuniko cha risasi

Hii inahusu kifuniko kizito. Risasi ni madini mazito.

kulikuwa na mwanamke chini yake amekaa ndani yake

Mwanamke asingeweza kutosha halisi ndani ya kikapu wa umbo hili.Japokuwa ono la Zakaria alitosha ndani ya kikapu. Mara nyingi maono ya maumbo ya vitu yanatiwa chumvi. Wote mwanamke na kikapu wanawakilisha mambo mengine.

Zechariah 5:8

Huu ni uovu

mwanamke anawakilisha uovu.

na upepo ulikuwa chini ya mbawa zao.

Kifungu hiki kinaeleza jinsi wanawake walivyotumia mbawa zao kuchukuliwa na upepo na kuruka.

walikuwa na mabawa kama mabawa ya korongo

Wanawake walikuwa na mbawa zilizoonekana kama za korongo. Huyu ni ndege mkubwa mwenye mabawa ya mita 2 hadi 4.

kati ya nchi na mbingu

Kikapu kiliinuliwa juu angani. Inasema "kati ya nchi na mbingu" kuvuta usikivu wao na kuonesha kikapu kilipokuwa kwa kwa kuwahusisha.

Zechariah 5:10

Wanapeleka wapi kikapu?

Wanawake wanapeleka wapi kikapu?

Ili kwamba hekalu litakapokuwa tiyari... katika msingi wake ulioandaliwa

"na wakati hekalu litakapokuwa tayari, kikapu kitawekwa mahali palipoandaliwa"

Zechariah 6

Zechariah 6:1

inua macho yangu

Hii inamaanisha kutazama katika jambo fulani.

milima miwili iliyokuwa imetengenezwa kwa shaba

"milima miwili ilikuwa ya shaba"

kibandawazi cha kwanza ... kibandawazi cha pili.

"kibandawazi cha 1... kibandawazi cha 2"

Zechariah 6:5

Hizi ni pepo nne za mbinguni

Malaika anaeleza kwamba vibandawazi pamoja na farasi vinawakilisha pepo nne za mbinguni.

pepo nne

Neno "pepo" linamaanisha pande nne: kaskazini, mashariki, kusini, na magharibi. Walakini, baadhi ya matoleo mapya yanafasiri maneno haya ya Kiebrania kumaanisha "roho nne."

farasi weupe wanakwenda nchi ya magharibi

baadhi ya matoleo mapya yanafasiri maneno haya ya Kiebrania kumaanisha "farasi weupe wanatoka baada yao."

Zechariah 6:7

Wakawatamama

"Kutazama farasi weusi"

Zechariah 6:9

neno la Yahwe lilikuja

"Yahwe alinena neno lake."

Heldai, Tobiya, na Yediya... Yehosadaki

Haya ni majina ya wanaume.

Kisha uchukue fedha na dhahabu, ufanye taji

"Kisha tumia fedha na dhahabu kufanya taji.

Yoshua mwana wa Yehosadaki

Huyu siyo yule aliyekuwa msaidizi wa Musa; huyu ni kuhani mkuu ambaye ametajwa katika kitabu cha Hagai.

Zechariah 6:12

Kuongea naye na kusema

"Yahwe alimwambia malaika ili aongee na Zakaria na kusema"

jina lake ni tawi

Malaika wa Yahwe anampa jina hili Yoshua mfalme mpya.

atakuwa

Kifungu "kukua" ni neno la picha la tawi kuanza kuchipua.

kuinua utukufu wake

Maana pendekezwa: 1) "kuongeza utukufu wa hekalu" au 2)"inua na kuvaa utukufu wa hekalu yeye mwenyewe kama mtu angeweza kuvaa nguo"

ufahamu wa amani utakuwa kati ya vyote viwili

"wajibu wake wa mfalme na kuhani utaunganishwa."

Zechariah 6:14

Taji itawekwa katika hekalu la Yahwe

"Nitaweka taji yangu katika hekalu langu"

Taji

Neno "taji" inamtaja mfalme kama ambavyo mfalme angevaa taji.

iliwekwa katika hekalu la Yahwe

Hii inahusu mfalme pia akiwa kuhani, kama kuhani anatumika hekaluni.

Heldai, Tobiya, na Yedaya

Haya ni majina ya wanaume

kama kumbukumbu ya ukarimu wa mwana wa Zefania

Baadhi ya matoleo ya kisasa yanafasiri kifungu hiki "kama kumbukumbu kwa Heni, mwana wa Zefania" au "kama kumbukumbu kwa mwenye neema, mwana wa Zefania." Pia, baadhi ya matoleo ya kisasa yanafasiri neno "Heni" kumaanisha jina "Yosia."

walioko mbali

Hii inawahusu Waisraeli waliokuwa wamesalia Babeli.

hivyo utajua

Neno "wewe" inamaanisha watu wa Israeli.

sikilizeni kweli

"sikilizeni kwa uaminifu"

Zechariah 7

Zechariah 7:1

Mfalme Dario alipokuwa mfalme kwa miaka nne.

"katika mwaka wa nne tangu Dario awe mfalme"

siku ya nne ya mwezi wa Kisleu(ndio mwezi wa tisa)

"Kisileu" ni mwezi wa tisa wa kalenda ya Kiebrania. Siku ya nne ni sawa na mwishoni mwa Novemba katika kalenda ya sasa.

neno la Yahwe lilikuja

"Yahwe alinena neno lake"

Shareza na Regemu Meleki

Haya ni majina ya wanaume.

walisema, "je! niomboleze... miaka?

Neno "wale" linamrejerea Shareza na Regemu Meleki.

katika mwezi wa tano

Wayaudu walifunga wakati wa sehemu ya mwezi wa tano wa kalenda ya Kiebrania kwa sababu huu ndio wakati Wababeli walipoliaribu hekalu la Yerusalemu. Mwezi wa tano ni wakati wa sehemu ya mwisho wa Julai na mwanzoni mwa Agosti katika kalenda ya sasa.

Zechariah 7:4

katika wa tano

"mwezi wa tano"

katika mwezi wa saba

Wayaudi waliomboleza wakati wa sehemu ya mwezi wa saba wa kalenda ya Kiebrania kwa sababu katika mwezi huu Wayaudi waliokuwa wamebaki Yerusalemu walikimbilia Misri baada ya kuuawa kwake Gedalia, ambaye mfalme wa Babeli alikuwa amemteua kuwa gavana juu ya Yuda. Mwezi wa saba ni wakati wa mwishoni mwa Septemba na mwanzoni mwa Oktoba katika kalenda ya sasa.

kwa miaka hii sabini

Watu wa Israeli walikuwa wamekuwa watumwa kwa miaka 70 huko Babeli.

mlipokula na kunywa

Kifungu hiki kinamaanisha walipokula na kunywa katika sherehe kuheshimu jinsi Yahwe alivyokuwa ameandaa kwa ajili yao.

Je ni kweli mlifunga kwa ajili yangu?

Swali linatumika kuwalaumu Waisraeli kwa kutomweshimu Yahwe walipofunga.

Je! hamkula na kunywa kwa ajili yenu wenywewe?

Swali linatumika kuwalaumu Waisraeli waliosherehekea sherehe kwa kutomweshimu Yahwe kwa sherehe zao.

Yahwe alisema kwa kinywa cha manabii wa zamani

Zakaria anarejerea manabii wa zamani kwa kurejerea sehemu ya mwili wao uliosema neno la Yahwe.

Haya hayakuwa maneno yaleyale... upande wa magharibi?

Swali hili laweza kuandikwa kama taarifa: "Haya yalikuwa maneno halisi yaleyale... upande wa magharibi."

Ilikaliwa

"waliishi ndani yake"

chini ya vilima

Hivi ni vilima kabla haujafika kwenye milima.

Zechariah 7:8

neno la Yahwe lilikuja

"Yahwe alinena neno lake."

Kila mtu na afanye hivi

Neno "hivi" inamaanisha jinsi mtu anavyopaswa kuhukumu.

mjane

mwanamke aliyefiwa mme

yatima

mtoto ambaye wazazi wake wamefariki

mgeni

Mtu aliyekatika nchi ya ugeni

kusiwa na mtu miongoni mwenu anayepanga madhara yoyote kinyume cha mwingine mioyoni mwenu.

"msifanye mipango ya kutenda uovu"

Zechariah 7:11

wakashupaza mabega yao

"walikuwa kama ng'ombe wanaokataa kuwekewa nira" au "walikuwa kama ng'ombe aliyekataa kutii"

waliziba masikio yao

"walikataa kusikia"

waliifanya migumu mioyo yao kama mwamba

"Walikataa kutii ujumbe wa Yahwe"

kwa kinywa cha manabii

"kupitia maneno ya manabii"

Zechariah 7:13

nitawatawanya kwa upepo wa kisurisuri

"nitawakusanya kamba kisurisuri kinavyosambaza majani"

kisurisuri

upepo wenye nguvu unaojisokota unaposafiri, ukisambaza vitu mbalimbali mahali pote.

Zechariah 8

Zechariah 8:1

Neno la Yahwe wa majeshi lilinijia kusema

Yahwe wa majeshi aliniambia

Nina huruma kwa ajili yake kwa hasira kubwa

"Nimejaa na hasira kwa ajili ya Sayuni"

mlima wa Yahwe wa majeshi

Hii inarejerea Mlima Sayuni.

Mlima mtakatifu

Hapa "Mtakatifu" yamaanisha "ni mali ya Yahwe."

Zechariah 8:4

iwe katika mitaa ya Yerusalemu

"kuwa inaishi Yerusalemu"

katika mikono yake kwa sababu amezeeka

Wasaa wa kuzeeka ni alama ya amani na mafanikio.

Na mitaa ya mji itajaa

Maeneo ya wazi ya mji yatakuwa yamejaa watu katika shughuli zao za kawaida.

Zechariah 8:6

Kama jambo haliwezekani katika mcho ya

"Ikiwa jambo fulani halionekani kuwezekana"

masalia ya watu hawa

"watu wa Yuda waliosalia"

Je! lisiwezekane pia machoni pangu?

Mungu anauliza swali hili ili kuwashawishi watu wake kuamini ahadi zake.

Hili ni tamko la Yahwe

Kifungu hiki kwa kawaida kimetafsiriwa kama "asema Yahwe. Kifungu hiki kimetumika mara nyingi katika kitabu cha Zakaria.

Ninaelekea kuwakomboa watu wangu

"Niko karibu kuwakomboa watu wangu walikwenda uamishoni"

Zechariah 8:9

Msingi wa nyumba yangu ulipowekwa

"Msingi wa nyumba yangu ulipowekwa mahali pake" kwa "mlipokuwa mkijenga msingi wa nyumba yangu"

Itieni nguvu mikono yenu

"fanyeni kazi kwa bidii"

Maana kabla ya siku hizo

"Kabla hamjaanza kulijenga hekalu"

Hakuna mazao yaliyokusanywa ndani

"hakukuwa na mazao ya kuvuna"

Hakukuwa na faida kwa mtu wala mnyama

Haikuwa na faida kwa mwanadamu na wanyama wao kuilima nchi, kwa sababu hawakupata chakula kutoka ndani yake.

Zechariah 8:11

kama siku za kale

"kama katika wakati uliopita"

Nitakuwa pamoja na masalia ya watu hawa

"Sasa nitawabariki watu hawa" au "Sasa nitawatendea watu hawa kwa upole"

mbegu ya amani itapandwa

"Nitawafanya kuwa katika amani"

Hili ni tamko la Yahwe

Kifungu hiki kwa kawaida kimetafsiriwa kama "asema Yahwe. Kifungu hiki kimetumika mara nyingi katika kitabu cha Zakaria.

nchi itatoa mazao yake

"kutakuwa na kuvuna kwema katika mashamba"

mbingu zitatoa umande wake

Umande kwa kawaida ilikuwa ni ishara ya mafanikio. Yaani "kuwatuwa na mvua nyingi"

kuyarithi yote haya

"kuwa na haya yote wakati wote"

Zechariah 8:13

Mlikuwa mfano wa laana kwa mataifa mengine

"Nilipowaadhibu, mataifa mengine yalijifunza"

Nyumba ya Yuda na nyumba ya Israeli

"Watu wa Yuda na Israeli"

Mikono yenu itiwe nguvu

"fanyeni kazi kwa bidii"

siwazuru

"kuwaadhibu"

kuchokoza hasira yangu

"kunikasirisha"

hakujuta

"hakuamua kuwaadhibu kidogo"

Zechariah 8:16

mnalopaswa kufanya

"Ninyi" inawarejerea watu wa Yuda.

Ongeeni kweli, kila mtu na jirani yake

"semeni kweli kwa kila mtu"

Hukumuni kwa kweli, haki, na amani malangoni penu

"Hukumuni kwa haki katika mahakama zenu ili watu waishi kwa amani.

wala msivutwe na nadhiri za uongo

Msikubaliane na watu wasemao uongo katika mashitaka mahakamani"

Hili ni tamko la Yahwe

Kifungu hiki kwa kawaida kimetafsiriwa kama "asema Yahwe. Kifungu hiki kimetumika mara nyingi katika kitabu cha Zakaria.

Zechariah 8:18

Kisha neno la Yahwe wa majeshi likanijia mimi

"Mimi" inamrejerea Zakaria.

Mfungo wa mwezi wa nne

Wayaudi waliomboleza katika kipindi cha sehemu ya mwezi wa nne wa kalenda ya Kiebrania kwa sababu huu ulikuwa wakati Wababeli walipovunja ukuta wa Yerusalemu. Mwezi wa nne ni wakati wa mwishoni mwa Juni na mwanzoni mwa Julai katika kalenda ya sasa.

mwezi wa tano

Wayaudu walifunga wakati wa sehemu ya mwezi wa tano wa kalenda ya Kiebrania kwa sababu huu ndio wakati Wababeli walipoliaribu hekalu la Yerusalemu. Mwezi wa tano ni wakati wa sehemu ya mwisho wa Julai na mwanzoni mwa Agosti katika kalenda ya sasa.

mwezi wa saba

Wayaudi waliomboleza wakati wa sehemu ya mwezi wa saba wa kalenda ya Kiebrania kwa sababu katika mwezi huu Wayaudi waliokuwa wamebaki Yerusalemu walikimbilia Misri baada ya kuuawa kwake Gedalia, ambaye mfalme wa Babeli alikuwa amemteua kuwa gavana juu ya Yuda. Mwezi wa saba ni wakati wa mwishoni mwa Septemba na mwanzoni mwa Oktoba katika kalenda ya sasa.

mwezi wa kumi

Wayaudi waliomboleza wakati wa sehemu ya mwezi wa kumi katika kalenda ya Kiebrania kwa sababu huu ni wakati Wababeli walipoanza kuuhsusu Yerusalemu. Mwezi wa kumi ni mwishoni mwa Desemba na mwanzoni mwa Januari katika kalenda ya Magharibi.

Zechariah 8:20

Watu watakuja tena

"Watu watakuja tena Yerusalemu"

Watu wengi na mataifa yenye nguvu yatakuja

"Watu wengi watakuja, wakiwemo kutoka mataifa makubwa"

Zechariah 8:23

watashika pindo la vazi lenu

"watashika mavazi yenu kuvuta makini yenu"

Na twende nanyi

"Tafadhari tusafiri pamoja nanyi kwenda Yerusalemu"

Mungu yu pamoja nanyi

"Mungu yu pamoja nanyi watu"

Zechariah 9

Zechariah 9:1

Hili ni tamko la neno la Yahwe kuhusu

"Huu ni ujumbe wa Yahwe kuhusu"

Nchi ya Hadraki na Dameski

"Watu wa nchi ya Hadraki na mji wa Dameski

Kwa maana jicho la Yahwe lipo juu ya watu wote

"Maana Yahwe anamwangalia kila mtu" Lakini, matoleo mengi ya kisasa yanafasiri kifungu hiki kama "macho ya watu" na ya wale wa makabila yote ya Israeli yanamwangalia Yahwe."

Hamathi

"Watu wa nchi ya Hamathi"

Tiro na Sidoni

"Watu wa Tiro na Sidoni"

japokuwa ni wenye hekima sana

Pengine Zakaria hakumaanisha hakika kwamba watu wa Hamathi walikuwa wenye hekima.

Zechariah 9:3

amejijengea ngome

Hapa mji wa Tiro umepewa picha kama ya mwanamke.

kurundika fedha kama mavumbi na dhahabu safi kama matope mitaani

"kukusanywa kwa dhahabu na fedha nyingi mitaana kama mchanga "

Tazama! Bwana atamnyang'anya

"Iweni tayari! Bwana atachukua miliki za Tiro"

na kuharibu nguvu zake juu ya bahari

"na kuharibu meli za Tiro ambazo watu wanazitumia kupigana juu ya bahani"

hivyo ataharibiwa na moto

"na kuuteketeza mji hata mavumbini"

Zechariah 9:5

taona

"ataona Tiro ikiharibiwa"

Wageni watafanya makazi yao katika Ashidodi

"Wageni wataichukua Ashidodi na kufanya makao yao pale"

nami nitakiondoa kiburi cha Wafilisiti

"Nitawafanya Wafilisita wasijivune tena"

Nitaondoa damu yao katika vinywa vyao na machukizo yao kutoka kati ya meno yao

Hii inamaanisha nyama pamoja na ndamu ndani, na nyama iliyotolewa kwa vinyago. Yaani "Sitawaruhusu tena kula nyama pamoja damu ndani yake, na nitawazui kula chakula kilichotolewa kwa sanamu"

Zechariah 9:8

Nitaweka kambi karibu na nchi yangu

Mungu anaongea juu yake kama alikuwa jeshi.

Zechariah 9:9

Piga kelele kwa furaha, ewe binti Sayuni! Piga kelele kwa shangwe, ewe binti Yerusalem!

Mistari hii miwili inamaanisha jambo moja na inazidisha agizo la kufurahi.

binti Sayuni... binti Yerusalem

"Sayuni" ndiyo "Yerusalemu." Nabii anauzungumzia mji kanakwamba ni binti.

juu ya punda, juu ya mwanapunda

Vifungu hivi viwili kimsingi vinamaanisa jambo moja na vinamrejerea mnyama mmoja. Mstari wa pili unaweka wazi kwamba huyu ni mwanapunda.

kukatilia mbali kibandawazi kutoka Efraimu

"Kuharibu vibandawazi vitumikavyo kwa vita katika Israeli"

farasi kutoka Yerusalemu

"farasi wa vita katika Yerusalemu"

upinda utakatiliwa mbali kutoka katika vita

Hapa upinde unawakilisha silaha zote zitumikazo kwa vita. "Silaha zote za vita zitateketezwa"

Maana atanena amani kwa mataifa

Hapa tendeo la kutangaza amani linawakilisha tendo la kufanya amani.

utawala wake utakuwa kutoka bahari hata bahari, na kutoka katika mto hadi miisho ya dunia

"ufalme wake utakuwa juu ya dunia yote!"

Zechariah 9:11

Lakini kwenu

Hapa "ninyi" inamaanisha watu wa Israeli.

shimo ambalo halina maji

Shimo hapa linawakilisha uhamisho.

Rudini ngomeni

"Rudini katika nchi yenu mahali mtakapokuwa salama"

wafungwa wa tumani

Hii inamaanisha Waisraeli waliokuwa kifungoni waliokuwa bado wanamatumaini kwamba Mungu atawakomboa.

pinda Yuda kama upinde wangu

Watu wa Yuda wanatajwa kama walikuwa upinde uliobebwa na Mungu kwa vita.

kulijaza podo langu kwa Efraimu

Watu wa Israeli, ufalme wa kaskazini, wanatajwa kama walikuwa mishale ambayo Mungu angewapigia adui zake. Podo ni mfuko unaotunza mishale ya askari.

Nimewainua wana wenu, Sayuni, kinyume cha wana wenu, Ugiriki,

Mungu anazungumza na watu wa mataifa mawili tofauti kwa wakati mmoja.

Zechariah 9:14

Maelezo ya Jumla:

Sehemu hii ya unabii inaendelea na maneno ya Hosea, badala ya maneno ya Yahwe yaliyonenwa kupitia kwake.

Ataonekana kwao

Neno "wao" linamaanisha watu wa Mungu. Yaweza pia kuwa "taonekana angani kwa watu wake" au "atakuja kwa watu wake"

tapiga kelele kama radi

Wakati mwingine Waisraeli walidhani miale ya radi kama mishale aliyopiga Mungu.

piga tarumbeta

Tarumbeta ilikuwa ni pembe ya kondoo. Watu waliipuliza kama ishara ya vita au matukio mengine.

ataendelea na dhuruba kutoka Temani

Wakati mwingine Waisraeli walifikiri kwamba Mungu alikuwa akisafiri kwa upepo wa tufani utokao kusini.

atararua

"kushinda kabisa"

kuyashinda mawe ya kombeo

Waisraeli watawashinda askari wanaopigana kwa kutumia kombeo. Askari hawa wanawakilisha adui wote wa Israeli, haijarishi silaha walizonazo.

Ndipo watakapo kunywa na kupiga kelele kama mtu aliyelewa kwa mvunyo

"Watapiga kelele na kusherehekea ushindi wao kwa kelele kama walikuwa wamelewa."

watajazwa kwa mvinyo kama mabakuli

Pengine inamaanisha mabakuli makuhani waliyotumia kubeba damu ya mnyama katika madhabahu.

kama pembe za madhabahu

Madhabahu zilikuwa na pembe damu zilipokusanywa.

Zechariah 9:16

Maelezo ya Jumla:

Zakaria anaendelea kuongea na watu.

Ndipo watakapo kunywa na kupiga kelele kama mtu aliyelewa kwa mvunyo

"katika nchi yetu watakuwa kama mawe mazuri katika taji"

vijana watastawi juu ya nafaka

Vijana wataishi kwa chakula wanachopata kutoka katika mavuno.

na bikra juu ya divai tamu

Mabinti watafurahia mvinyo mpya. Hizi ni rejea kwa vijana wa kiume na kike wakiwakilisha hesabu ya watu wote wa Israeli

Zechariah 10

Zechariah 10:1

Maelezo ya Jumla:

Zakaria anaenelea kuongea na watu.

hufanya mvua ya miunguromo na dhoruba

"hufanya mawingu ya dhoruba"

sanamu uongea kwa uongo

"sanamu zinatoa ujumbe wa uongo"

waganga hunena uongo

"waganga wanaona maono ya uongo"

wanasema ndoto za udanganyifu

"waganga wanasema uongo kuhusu ndoto zao ili kuwadanganya watu"

wanapotea kama kondoo

"watu hawajui njia ya kufuata"

Zechariah 10:3

Gadhabu yangu inawaka dhidi ya wachungaji

"Wachungaji" wanawakilisha viongozi wa watu wa Mungu.

ni mabeberu - viongozi - nitakao waadhibu

"Mabeberu" wanawakilisha viongozi wasiofaa

Yahwe wa majeshi atalihudumia pia kundi la kondoo wake, nyumba ya Yuda

"Nitaiangalia nyumba ya Yuda"

kuwafanya kama farasi wake wa vita!

"Tawapa uwezo wangu wa nguvu isiyoogopesha"

Zechariah 10:4

Kutoka kwao litatoka jiwe kuu la pembeni

"Jiwe la pembeni litatoka kwao." Kiongozi mhimu anazungumzwa kama vile jiwe kuu la msingi wa jengo.

kutoka kwao kitatoka kigingi cha hema

"kigingi cha hema kitatoka kwao." Viongozi wakuu wanazungumzwa kama vile vigingi vikubwa vinavyolishikilia hema mahali pake.

kutoka kwao utatoka upinde wa vita

"upinde wa vita utatoka kwao." Viongozi wa kijeshi wanasemwa kama walikuwa upinde uliotumiwa vitani.

Watakuwa kama mashujaa

"Watakuwa wenye nguvu vitani"

wawakanyagao adui zao katika matope ya mitaani vitani

"wawashindao adui zao kwa ukamilifu"

nao watawaabisha wapanda farasi

"nao watawashinda adui zao wapiganao nao katika farasi"

Zechariah 10:6

Nitaitia nguvu nyumba ya Yuda

"Nitawaimarisha watu wa Yuda"

nyumba ya Yusufu

Hii inamaanisha watu wa ufalme wa Israeli kaskazini.

nilikuwa sijawaondoa

"Nilikuwa sijawakataa"

Efraimu atakapokuwa kama shujaa

"Efraimu" inarejerea ufalme wa Israeli ya kaskazini.

mioyo yao itafurahi kama kwa mvinyo

"nao watakuwa kweli na furaha sana

wana wao wataona na kufurahi. Mioyo yao itanifurahia!

"Wana wao wataona yaliyotokea na watafurahi kwa sababu ya yale Yahwe aliyowafanyia!

Zechariah 10:8

Nitawanong'oneza

kunong'oneza ni kutoa sauti ya juu, nyembamba kupitia midomo iliyominywa. Kwa kawaida hutolea kuwapa wengine ishara,

mpaka kutakapokuwa hakuna nafasi tena kwa ajili yao

Watu wataendelea kwenda Yuda na itajazwa watu hata kusiwe na nafasi ya watu kuishi pale tena.

Zechariah 10:11

Nitapita katika bahari ya mateso yao

Maandiko mara nyingi urejerea bahari kama picha ya shida na magumu mengi.

na nitavikausha vilindi vyote vya Nile

"Nitaufanya Mto Nile kukauka"

Utukufu wa Ashuru utashushwa chini

Hapa "utukufu wa Ashuru" pengine unamaanisha jeshi la Ashuru.

na fimbo ya Misri itakwenda mbali kutoka kwa Wamisri

"na nguvu ya Misri kutawala mataifa mengine itakwisha."

hili ni tamko la Yahwe wa majeshi

Kifungu hiki mara kwa mara kinafasiriwa kama "asema Yahwe" Kifungu hiki kimetumika mara nyingi katika kitabu cha Zakaria.

Zechariah 11

Zechariah 11:1

Fungua milango yako, ee Lebanoni, ili moto uteketeze mielezi yako

Nabii anaongeza na nchi ya Lebaboni kama vile alikuwa ni mtu.

Omboleza, enyi miti ya misonobari, kwani mierezi imeanguka

"Ikiwa miti ilikuwa watu, ingelia kwa huzuni. Misonobari imebaki pekee kwa sababu mierezi imechomwa na kuanguka."

Ombolezeni, enyi mialoni ya Bashani, kwani msitu wenye nguvu umeshushwa.

"Ikiwa miti ya mialoni iliyoko Bashani ingekuwa watu, wangeomboleza, kwani msitu mzito umeangushwa."

Wachungaji wanapiga yowe

"Wachungaji wanalia kwa sauti"

kwa kuwa utukufu wao umeharibiwa

"Utukufu wao" pengine inawakilisha nyasi nyingi ambapo wachungaji walipeleka kondoo wao.

kwa kuwa kiburi cha Mto Yordani

"kwa sababu miti walipokaa kando ya Mto Yordani imeharibiwa."

Zechariah 11:4

Maelezo ya Jumla:

Hapa Yahwe anaanza kutoa maelekezo kwa Zakaria katika muundo wa mfano kuhusu wachungaji na kondoo.

wenyeji wa nchi

"watu wa nchi"

hivi ndivyo asemavyo Yahwe

Kifungu hiki mara kwa mara kinafasiriwa kama "asema Yahwe" Kifungu hiki kimetumika mara nyingi katika kitabu cha Zakaria.

kumwelekeza kila mtu katika mkono wa jirani yake

"kumfanya kila mtu kutawaliwa na mtu mwingine"

katika mkono wa mfalme wake

"katika utawala usio wa haki wa mfalme wake"

wataiharibu nchi

"hawatakuwa na huruma juu ya watu wa nchi"

hakuna hata mmoja wao nitakayemwokoa kutoka katika mkono wao

"lakini sitawaokoa watu wa Yuda kutoka katika nguvu zao"

Zechariah 11:7

Maelezo ya Jumla:

mfana kuhusu wachungaji na kondoo unaendelea.

kondoo walioamriwa kuchinjwa

"kundi la kondoo waliokuwa wamekusudiwa kuchinjwa"

gongo

gongo ni miti inayotumika kwa makusudi mbalimbali, ikiwemo kuwaongoza watu. Yaweza kuwa na aina mbalimbali za ncha.

upendeleo

Matoleo mbalimbali yanafasiri neno la Kiebrania katika mazingira haya kama "neema" na "uzuri"

Umoja

Hili ni wazo la udugu kati ya sehemu mbili za Israeli, ufalme wa kaskazini na ufalme wa kusini.

sikuwavumilia tena

"Sikuweza kuwavumilia tena wenye kondooo waliokuwa wamewaajiri"

Zechariah 11:10

Maelezo ya Jumla:

Mfano wa wachungaji na kondoo unaendelea

nikaivunja kuvunja agano nililokuwa nimelifanya na kabila zangu zote

Hapa nabii anaongea na kutenda kama Yahwe.

amesema

"alikuwa amesema kwao ujumbe"

vipande thelathini vya fedha

gramu 330 za fedha. Shekeli ilikuwa na uzito wa gramu kumi na moja.

Zechariah 11:13

Maelezo ya Jumla:

Mfano kuhusu wachungaji na kondoo unaendelea

hazina

vyumba vya kuhifadhi vitu katika hekalu la Yahwe

thamani nzuri zaidi

Hii inamaanisha kwamba thamani hii ilikuwa ndogo sana kwa mchungaji aliyekuwa akaifanya kazi ya Yahwe.

vipande thelathini vya fedha

gramu 330 za fedha. Shekeli ilikuwa na uzito wa gramu kumi na moja.

Zechariah 11:15

Maelezo ya Jumla:

Mfano wa wachungaji na kondoo unaendelea.

kondoo walionona

Kondoo mwenyew afya, aliyekua vizuri.

atapasua kwato zao

pengine kama tendo la ukatili

Zechariah 11:17

Maelezo ya Jumla:

Mfano wa wachungaji na kondoo unaendelea.

Ole kwa wachungaji wasiofaa

"Huzuni ya namna gani inamsubiri mchungaji huyu asiyefaa"

uje dhidi ya mkono wake na jicho lake la kulia

"jereha mkono wa kulia na kuchomwa jicho la kulia"

Upanga na uje dhidi ya

"upanga" hapa unawakilisha adui watakao mshambulia mchungaji

mkono wake

nguvu ya kupigana

jicho lake la kulia

uwezo wa kuona wakati akipigana.

Zechariah 12

Zechariah 12:1

Maelezo ya Jumla:

Mistari hii inaanza sehemu inayozungumzia shambulio lijalo dhidi ya Yerusalemu na jinsi Mungu atakavyouokoa mji.

tamko la neno la Yahwe

Kifungu hiki mara kwa mara kinafasiriwa kama "asema Yahwe" Kifungu hiki kimetumika mara nyingi katika kitabu cha Zakaria.

azitandaye mbingu

"aliyeumba anga"

kuweka msingi wa dunia

"kuiweka dunia yote mahali pake"

aiumbaye roho ya mtu ndani yake

"aliumba roho ya mtu"

kikombe

"kikombe cha kitu cha kunywa"

kiwafadhaishacho watu wote wamzungukao

Hii ni, kinywaji ni pombe itakayowafanya majeshi wanaoishambulia Yerusalemu kulewa na kushindwa kupigana.

yeye

Huo ni, mji wa Yerusalemu. Ilikuwa kawaida kwa kiebrania kuzungumzia mji au nchi kama ni mwanamke.

jiwe zito kwa watu wa jamaa zot

"kisichowezekana kuondolewa"

Zechariah 12:4

Maelezo ya Jumla:

Mistari hii inaendelea na sehemu inayozungumzia shambulio lijalo dhidi ya Yerusalemu na jinsi Mungu atakavyouokoa mji.

siku hiyo

Siku majeshi yatakapoishambulia Yerusalemu.

Hili ni tamko la Yahwe

Kifungu hiki mara kwa mara kinafasiriwa kama "asema Yahwe" Kifungu hiki kimetumika mara nyingi katika kitabu cha Zakaria.

Nitaiangalia kwa upendeleo

"Nitailinda"

nyumba ya Yuda

"watu wa Yuda"

wasema mioyoni mwao

Inamaanisha kwamba watafikiri na kujisemea wenyewe.

kwa sababu wa Yahwe wa majeshi

"kwa sababu wanamwabudu Yahwe wa majeshi"

Zechariah 12:6

Maelezo ya Jumla:

Mistari hii inaendelea na sehemu inayozungumzia shambulio lijalo dhidi ya Yerusalemu na jinsi Mungu atakavyouokoa mji.

siku hiyo

Hii inamaanisha wakati Yerusalemu itakaposhambuliwa na Mungu uwashinda adui zake.

kama mitungi ya moto katika miti... nafaka iliyosimama

kama mitungi ya moto kati ya mabua ya nafaka yasiyovunwa shambani"

vyungu vya moto

Kitu ambacho watu wa kale walitumia kubebea makaa ya moto.

miale ya moto

Ukuni unaowaka upande mmoja unaotoa nuru mtu anapotembea au kuchukua moto mahali fulani.

utateketeza watu wote walio karibu

"nitawaharibu watu wawazungukao"

Yerusalemu atakaa mahali pake tena

Watu wa Yerusalemu wataishi tena katika mji wao.

Zechariah 12:7

Maelezo ya Jumla:

Mistari hii inaendelea na sehemu inayozungumzia shambulio lijalo dhidi ya Yerusalemu na jinsi Mungu atakavyouokoa mji.

hema za Yuda

Hapa "hema" uwakilisha nyumbani, na nyumba zinawawakilisha watu wanaoishi ndani yake.

nyumba ya Daudi

Maana pendekezwa 1) wazao wa Daudi au 2) daraja la watawala.

malaika wa Yahwe

Huyu ni malaika wa Yahwe aliyetumwa kuwalinda watu.

Zechariah 12:10

nitamwaga roho ya huruma na kuiombea

"Nitawapa watu roho ya rehema kwa wengine na kuniombwa rehema"

waliyemchoma

"waliyemwua kwa mchoma"

maombolezo huko Yerusalemu yatakuwa kama maombolezo ya Hadadi Rimoni

Hadadi Rimoni yaweza kuwa ni sehemu ambapo Mfalme mwema Yosia alikufa vitani baada ya kujeruhiwa katika Vita ya Megido. Inaonekana kwamba baadaya yalitokea mapokeo ya kuomboleza kwa ajili ya kifo chake pale. Baadhi ya watu, lakini wanafikiri kwamba Hadadi Rimoni ililikuwa jina la mungu wa uongo aliyeaminiwa kufa kila mwaka, tukio ambalo wafuasi wake wangekwenda kumwombolezea.

Megido

Hili ni jina la tambarare katika Israeli.

Zechariah 12:12

Nchi

Hii inawahusu watu wote waliokuwa wanaishi katika nchi ya Yuda.

Nyumba ya Daudi... ya Nathani... ya Lawi

Wazao wa Daudi... wa Nathani ... wa Lawi.

Zechariah 13

Zechariah 13:1

kijito

Mahali ambapo kwa asili maji yanatiririka kutoka ardhini.

kwa ajili ya dhambi zao na uchafu

"Kutakasa dhambi na uchafu wao"

hili ni tamko la Yahwe wa majeshi

Kifungu hiki mara kwa mara kinafasiriwa kama "asema Yahwe" Kifungu hiki kimetumika mara nyingi katika kitabu cha Zakaria.

kuondoa majina ya sanamu katika nchi

kufuta ibada ya sanamu katika nchi yote"

Nitawaondoa pia katika nchi manabii wa uongo na roho wao mchafu

"Pia nitaondoa manabii wa uongo na roho wao wachavu katika nchi."

Zechariah 13:3

baba yake na mama yake waliomzaa

Kifungu "waliomzaa" kinaelezea "baba yake na mama yake" ili kuonesha mshangao kwamba wazazi wangemtendea hivi mwanao.

Hautaishi

Lazima ufe"

watamchoma

Kumchoma ili kumwua."

Zechariah 13:4

kwamba kila nabii

Inawahusu manabii wa uongo siyo manabii wa Yahwe.

hawatavaa tena vazi la singa

"vazi" linalotajwa hapa ni lile zito la nje. Lililotengenezwa kwa manyoya ya wanyama lililovaliwa na manabii.

kuilima ardhi

Hili ni "shamba"

ardhi ndiyo kazi yangu tangu ujana wangu

Baadhi ya matoleo ya kisasa yanafasiri sehemu hii kama "mtu alinipata tangu ujana wangu," yaani, kumpata kama mtumishi.

Majeraha haya katika mikono yako ni nini?

"Ulipataje majeraha hayo katika kifua chako? hii inamaanisha kwa desturi ya kawaida kwa manabii wa uongo kujidhuru wenyewe katika sherehe zao.

atajibu

Hii ni , atajibu kwa uongo.

Zechariah 13:7

Upanga! inuka mwenyewe

"wewe, upanga! Unapaswa kuamka." Hii ni amri kutoka kwa Yahwe kwa mchungaji wake kupigwa na kuawa.

dhidi ya mchungaji wangu

Hii inamaanisha mfalme fulani au mtumishi fulani wa Yahwe.

hivi ndivyo asemavyo Yahwe wa majeshi

Kifungu hiki mara kwa mara kinafasiriwa kama "asema Yahwe" Kifungu hiki kimetumika mara nyingi katika kitabu cha Zakaria.

kondoo

"Kondoo" ni watu wa Israeli.

wadogo

Pengine inarejerea kwa Waisraeli wote walio dhaifu na bila ulinzi.

Zechariah 13:8

hili ni tamko la Yahwe

Kifungu hiki mara kwa mara kinafasiriwa kama "asema Yahwe" Kifungu hiki kimetumika mara nyingi katika kitabu cha Zakaria.

Nitaipitisha theluthi katika moto

Madini yanapitishwa motono ili kusafishwa au kuboreshwa. Hii inaonesha watu wakipata mateso ili kwamba wawe waaminifu zaidi kwa Mungu.

kuwasafisha kama fedha isafishwavyo; nitawajaribu kama dhahabu ijaribiwavyo

Kusafisha inamaanisha kufanya madini ya thamani kama vile fedha safi zaidi. Madini kama vile fedha na dhahabu yanajaribiwa ili kuona jinsi yalivyosafi au na nguvu. Haya yote yanatumika kuwafanya watu kuwa waaminifu zaidi kwa Mungu.

Zechariah 14

Zechariah 14:1

Maelezo ya Jumla:

Sura hii inaelezea vita ya mwisho kwa mji wa Yerusalemu na jinsi Mungu atakavyouokoa.

mateka wenu watakapogawanywa katikati yenu

Inamaanisha "Adui zenu watachukua mali yenu yote na kuigawana mbele yenu"

nitayakusanya mataifa yote kinyume cha Yerusalemu kwa vita

"Nitayafanya mataifa kuishambulia Yerusalemu"

kumbukumbu ya watu haitaondolewa mjini

"Adui zenu wataacha masalia kukaa katika mji"

Zechariah 14:3

Maelezo ya Jumla:

Mistari hii inaelezea vita ya mwisho kwa mji wa Yerusalemu na jinsi Mungu atakavyouokoa

kama apigavyo vita katika siku ya vita

"Kama alivyopiga vita zamani"

miguu yake itasimama juu ya Mlima wa Mizeitun

"Miguu yake" inamtaja Yahwe mwenyewe.

Zechariah 14:5

Maelezo ya Jumla:

Mistari hii inaelezea vita ya mwisho kwa mji wa Yerusalemu na jinsi Mungu atakavyouokoa

Azali

Hili ni jina la mji au kijiji mashariki ya Yerusalemu.

watakatifu

Pengine hii inataja malaika wa Mungu.

Zechariah 14:6

Maelezo ya Jumla:

Mistari hii inaelezea vita ya mwisho kwa mji wa Yerusalemu na jinsi Mungu atakavyouokoa.

maji yaliyohai

Kwa kawaida hii inamaanisha maji yatiririkayo, tofauti na maji yaliyotuama.

bahari ya mashariki

Hii inamaanisha Bahari ya chumvi, iliyomashariki mwa Yerusalemu.

bahari ya magharibi

Hii inamaanisha bahari ya Mediterania.

Zechariah 14:9

Maelezo ya Jumla:

Mistari hii inaelezea vita ya mwisho kwa mji wa Yerusalemu na jinsi Mungu atakavyouokoa.

kutakuwa na Yahwe, Mungu mmoja, na jina lake pekee

"kutakuwa na Mungu mmoja pekee, Yahwe, atakayeabudiwa"

Araba... Geba... Rimoni

Haya ni majina ya maeneo

Yerusalemu itaendelea kuwa juu

Hii inamaanisha mwinuko wa mji wa Yerusalemu, kama mita 760 juu ya usawa wa bahari.

Yeye

Yerusalemu na miji mingine imetajwa kwa kiwakilishi cha jina la kike(she)

ataishi mahali pake mwenyewe

"ataishi mahali amekuwa akiishi daima"

lango la Benjamini... lango la kwanza... Lango la pembeni

Haya ni majina mbalimbali ya malango katika ukuta wa Yerusalemu.

Mnara wa Hananeli

Hii inamaanisha sehemu yenye nguvu katika ulinzi wa mji ukutani. Pengine ulijengwa na mtu aliyeitwa Hananeli.

shinikizo la mfalme

Pengine inamaanisha mahali mvinyo wa familia ya kifalme ulipotengenezewa.

Zechariah 14:12

Maelezo ya Jumla:

Mistari hii inaelezea vita ya mwisho kwa mji wa Yerusalemu na jinsi Mungu atakavyouokoa

wamesimama katika miguu yao

"kutembea tembea"

na mkono wa mwingine utainuliwa kinyume cha mkono wa mwenzake

Kila mtu atamshambulia mwenzake.

Zechariah 14:14

Maelezo ya Jumla:

Mistari hii inaelezea vita ya mwisho kwa mji wa Yerusalemu na jinsi Mungu atakavyouokoa.

Yuda atapigana pia na Yerusalemu.

Baadhi ya matoleo yanasomeka, "Yuda pia atapigana kwa ajili ya Yerusalemu." Nakala ya Kiebrania haiko wazi.

Watakusanya utajiri

"Watateka mali"

kwa wingi

"kwa kiwango kungi"

Zechariah 14:16

Maelezo ya Jumla:

Mistari hii inaelezea vita ya mwisho kwa mji wa Yerusalemu na jinsi Mungu atakavyouokoa

akaenda kinyume cha Yerusalemu

"Iliyoishambulia Yerusalemu"

itashambulia mataifa

"itaadhibu mataifa kwa ukali"

Zechariah 14:19

Maelezo ya Jumla:

Mistari hii inaelezea vita ya mwisho kwa mji wa Yerusalemu na jinsi Mungu atakavyouokoa

Zechariah 14:20

Maelezo ya Jumla:

Mistari hii inaelezea vita ya mwisho kwa mji wa Yerusalemu na jinsi Mungu atakavyouokoa

yatakuwa kama mabakuri mbele ya madhabahu

"Itakuwa takatifu kama mabakuri yaliyotumika madhabahuni"

kila chungu katika Yerusalemu na Yuda kitatengwa kwa ajili ya Yahwe wa majeshi

Aina mbalimbali ya vyungu na vifaa vingine vilifanywa maalumu ili kutumika hekaluni kwa ajili ya kumwabudu Yahwe na kwa sadaka. Vilikuwa maalumu, havikutumika kwa jambo lingine lolote.

Hakutakuwa na wafanyabiashara tena katika nyumba ya Yahwe wa majeshi

Ilikuwa ni desturi kwa wafanyabiashara kuwauzia watu vitu walivyoviitaji kwa ajili ya ibada ya Yahwe hekaluni. Baadhi ya tafasiri zina "Wakanaani" badala, kwa maana nakala ya Kiebrania yaweza kuwa na maana mbili: "wafanyabiashara" na "Wakanaani."

Malachi 1

Malachi 1:1

Agizo la neno la Bwana kwa Israel kwa Mkono wa Malaki.

"Bwana alizungumza haya maneno kwa waisrael kupitia Malaki"

Kwa mkono wa Malaki

kupitia kutenda kwa Malaki

Lakini wasema, "Umetupenda kwa namna gani?"

Hili swali linaonyesha shaka, au maswali juu ya ukweli wa neno la Mungu. Mungu anatumia swali kuwakemea watu. Tafsiri mbadala: lakini wasema, "Hujatupenda!"

Hakuwa Esau ndugu yake Yakobo?

"Nitawaambia jinsi ninavyowapenda ninyi. mnajua kwamba Esau ni ndugu yake Yakobo."

Asema Bwana

Bwana mwenye kweli amesema haya"

Nimempenda Yakobo

Bwana alichagua kuwa na mahusiano na Yakobo na kuwa Mungu ya Yakobo.

Nimemchukia Esau

Bwana alimkataa Esau

Nimeifanya Milima yake kuwa ya uharibifu na kuteketezwa

"Nimeifanya milima yake kuwa haifai kukaa ndani yake"

Na nimeufanya urithi wake kuwa sehemu ya mbweha wa mwituni

"Na nimeifanya nchi anayorithi kuwa jangwa ambapo wanyama pekee wanaweza kuishi"

Malachi 1:4

Kama Edom akisema

'Kama watu wa Edomu wakisema."

lakini nitawaangusha chini

"Nitaiangamiza"

na wanaume watawaita

"na wanaume wa taifa lingine watawaita"

nchi ya uovu

"nchi ya watu waovu

Macho yako yataona hiki

"Utaona hiki kikitokea'; hii ni kuwa, hawatahitaji mtu yeyote kuwaambia kilichotokea.

Malachi 1:6

mnadharau jina langu

"mmenifanyia kama mnayenichukia"

Lakini mwasema, 'ni kwa namna gani tumekudharau?

"ninyi makuhani mnasema, 'je tumekutendeaje kama tuna kuchukia? Tafsiri zingine zinasema: Mnanidharau lakini mwasema hapana!"

Mkate ulio najisi.

chakula ambacho hakikubaliki kwa dhabihu

Na mnasema, 'Tunakunajisi kwa namna gani?'

Tafsiri nyingine: Mnadhani mmekubalika kwangu lakini sivyo.

Malachi 1:8

Unapotoa wanyama vipofu kwa ajili ya kuteketezwa, huo sio uovu?

mnajua vizuri sana kuwa ni dhambi kutoa wanyama vipofu kwa ajili ya sadaka ya kutekezwa.

Na mtakapotoa vilivyo vilema na vigonjwa, hiyo siyo uovu?

Na mnajua vizuri sana kwamba ni dhambi kutoa vilivyo vilema na vigonjwa!"

Toa zawadi kwa watawala wenu; atawakubali au atawahurumia tu?

Hamwezi kutoa zawadi mbele ya watawala wenu! kama mlifanya, mnajua kabisa hawezi kukubali au kuwahurumia.

Zawadi

kutoa kama zawadi kuonyesha heshima

Na sas,... ni neema kwetu

Malaki hazungumzii kwa ajili ya Mungu. Anazunguza moja kwa moja kwa wasraeli.

Pamoja sadaka ya namna hii kwa sehemu yenu, atapokea aina yeyote?

"Unapotoa kile kisichoruhusiwa, Mungu atafurahishwa na ninyi?" hii ni kukemea. "Kama utatoa sadaka iliyokataliwa Mungu hakika Mungu hatakuwa na furaha na ninyi!"

Malachi 1:10

Oh, kama pekee

Hii inaelezea hisia kubwa.

ili kwamba msiwe mnawasha moto juu ya madhabahu yangu bure

"ili kwamba msitengeneze moto kuteketeza sadaka na dhambi kwa kutoa sadaka zisizo na maana"

Kutoka mikononi mwenu

"Kutoka kwenu"

jina langu

"mimi"

Kutoa mawio ya jua mpaka machweo yake

"Kila mahali," Sambamba na"Katika mataifa" na "kila sehemu"

Jina langu ni kuu katika mataifa

"Nitaheshimika katika mataifa yote"

kila sehemu uvumba utafukizwa kwa jina langu

"katika mataifa haya watu watafukiza uvumba kwa ajili yangu katika ibada"

Malachi 1:13

anaye koroma

kuonyesha kutoheshimu kwa kupiga kelele kupitia pua

Nitaikubali hii kutoka kwenye mikono yenu?"

nitaikubali hii kutoka kwenu? hii ni kukemea. Tafsiri zingine : "Sitakuba hakika hii kutoka kwenu!"

Alaaniwe mwenye kudanganya, mwenye mnyama dume katika kundi lake na akaapa kumtoa kwa kwangu

"Nitalaani vitu viovu kwa yeyote anayedanganya kwangu ambaye anaye mnyamna mkamilifu katika zizi lake na anaahidi kumtoa kama sadaka "

na hajatoa kwangu, Bwana, ambayo ni ujanja ujanja

"na pia dhabihu kwangu, Bwana, na mnyama ambaye hayuko imara"

Malachi 2

Malachi 2:1

liweke moyoni

"Fanya kuwa la Muhimu"

Malachi 2:3

Nitapaka mavi katika nyuso zenu

"Nitawaendesha ninyi bila heshima"

Mtachukuliwa mbali nayo

"watawatupa ninyi juu ya rundo la mavi"

Lawi

Yehova asema juu ya kabila la Lawi ingawa ni mtu mkoja

Malachi 2:5

Agano langu pamoja naye ilikuwa ni juu ya yhai na amani

"Kusudi la agano langu pamoja na Lawi ilikuwa ni juu ya makuhani kuishi maisha ya ushindi na amani"

Nilitoa hivi vitu kwake ili kuonyesha heshima kwa ajili yangu

Nilitoa vitu hivi kwake ili kwamba aniheshimu"

midomo

uwezo wa kuongea na kujulisha watu

ulinzi

"Kuhifadhi"

Malachi 2:8

"kudharauliwa na uovu mbele za watu

"Watu wamechukia na hawawaheshimu makuhani."

mmeonyesha upendeleo katika maelezo yenu.

"makuhani walionyesha tabia yakawaida kwa watu waliyoyapenda na hali ya ugumu wa tabia kwa watu ambayo hawakuipenda."

Malachi 2:10

Sisi sote hatuna baba mmoja? Hatuna Mungu mmumbaji mmoja?

"haya Maswali ni kuonyesha kukemea. "Sisi sote kwa hakika tunaye baba mmoja, Mungu wetu aliyetuumba sisi!"

Kwa nini tuna hila kila mmoja na ndugu yake, na kulikufuru agano la baba zetu?

hii pia ni kukemea. Hatupaswi hakika kuwatendea ndugu zetu na kutokuheshimu agano la Mungu na kutotii amri zake!"

mnafanya hila

kutomtii Mungu

Kwa ajili ya Yuda ameliharifu mahali patakatifu pa Bwana

"Wanaume wa Yuda hawakutii hekalu la Mungu"

na ameoa binti wa mungu mgeni

"na wameoa wanawake kutoka katika mataifa yanayoabudu miungu."

kila ukoo wa mtu ambaye amefanya haya

"Kila watoto na wajukuu wa mtu yeyote aliyefanya haya"

hata mmoja aliyeleta sadaka kwa Bwana wa majeshi

"hata kama mtu wa dhambi akileta sadaka kwa Mungu lakini hakutubu dhambi zake"

Malachi 2:13

akilia na kuugua

Maneno "Kilio" na "Kuugua" yanachangia maana moja yanakazia uimara wa kulia. "na kilio kikuu"

kutoka mikononi mwako

"Kutoka kwako"

Malachi 2:14

amefunika mavazi yake kwa vurugu

ni vurugu tu

Jilindeni ninyi kwa ninyi katika roho na kutokuwa na uaminifu.

"Kwa hiyo uamue kabisa kuwa mwaminifu kwa mke wako!"

Malachi 2:17

Mkisema

"kuwapotoisha wengine kwa kusema"

Yuko wapi Mungu wa haki?

Makuhani wanamkemea Mungu. "Mungu kwa hakika hakuonyesha haki kwa watu waovu!"

Malachi 3

Malachi 3:1

Nani atavumilia siku ya kuja kwake? na nani atasimama akionekana?

"Kwa hakika hakuna hata mmoja atakayekuwa na uwezo wa kumsaidia Bwana.

Kwa kuwa n yeye ni kama asafishaye kwa moto na kama sabuni ya kufulia.

Mungu analinganisha uwezo wake wa kutawala watu na kuwasafisha kutoka dhambini kwenda kwenye sabuni yenye nguvu kusafisha au nguvu ya moto unavyoyeyusha kitu. hii ni njia nyingine ya kusema kuwa Nguvu ya Mungu ya kufanya kitu haizuiliwi.

na atawasafisha wana wa Lawi

"na atawakusanyana kuwasafisha wana wa Lawi kutoka dhambini"

atawaboresha na kuwa kama dhahabuau shaba

Mungu ataondoa thambi kutoka kwa walawi na kuwafanya kuwa safi zaidi.

na wataleta sadaka ya haki kwa Bwana

"Na wataleta sadaka ya ibada iliyokubalika kwa Bwana"

Malachi 3:4

siku za kale, na miaka ya zamani

hizi aya mbili kimsingi zina maana mojana zinasisitiza kuwa sadaka zilipaswa kumpendeza Bwana. "kama ilivyokuwa huko nyuma."

karibia

"Sogea karibu"

Usimwonee mfanya kazi katikamshahara wake

"Usimlipe mfanyakazo mshahara kutokana na yeye alivyo"

kumweka mbali mgeni kutoka kwenye haki zake

kukataa wageni kuishi kwenye jamii ambayo ni haki kila mtu anapata.

Malachi 3:6

tokea siku za baba zenu mmegeuka kwingine na kuiacha amri na hamkuitunza

"Hamkutii amri zangu toka kipindi cha mababu zenu"

Tutakurudiaje?

"Hatujaenda mbali na wewe, kwa hiyo hatuwezi kurudi kwako."

Malachi 3:8

Mwanadamu atamwibia Mungu?

hii ni kukemea. Mwanadamu hakika hawezi kumwibiaMungu

Malachi 3:10

zaka kamili

"Zaka zote"

nyumba yangu

"hekalu langu"

Nijarinuni sasa katika hili...kama sitafungua kwa ajili yenu madirisha ya Mbinguni

"Kama mtanijaribu...Nitafungua madirisha ya mbinguni"

nitamkemea alaye

nitazuia wadudu na magonjwa

Malachi 3:13

walimjaribu Mungu na kujiepusha

walijaribu kumfanya akasirike, lakini hakuwahukumu"

Malachi 3:16

na kitabu cha kumbukumbu kilikuwa kimeandikwa mbele zake waliomwogopa Bwana

Hii inaweza kumaanisha 1) Waisrael waliandika kitabu ambacho wangekumbuka kile walichokuwa wameahidina kwa majina ya watu wenye hofu na Bwana au 2) Bwana alimfanya mtu flani huko mbinguni kuandika kitabu kikiwa na majina ya wale wanaomwogopa Bwana.

kitabu cha kumbukumbu

kitabu cha kuwasaidia watu kukumbuka mambo muhimu

heshimu jina lake

kumheshimu yeye

Malachi 3:17

watakuwa wangu

"Watakuwa watu wangu"

miliki yangu mwenyewe

"Hazina yangu maalumu"

Nitatenda

"Nahukumu"

kutofautisha kati ya

tazama tofauti kati ya au nitawaongoza kwa tofauti

Malachi 4

Malachi 4:1

tazama

"angalia" au "sikiliza" au "Uwe makini kwa kile nataka kuakuambia"

siku inakuja, ikiwaka kama tanuru

"siku ya hukumu inakuja, ni nitawahukumu watu waovu kama mkulima anavyochoma makapi na majani"

majivuno...waharifu

Tafsiri kama ulivyofanya "Kiburi" na "waharifu"

watakuwa mabua

"choma kama mimea mikavu"

Siku inayokuja itawachoma wote

"katika siku hiyo nitawachomawote"

sitaacha mzizi wala tawi

"hakuna kitakachobaki'

Jua la wenye haki litawainukia likiwa na uponyaji katika mbawa zake

Hii inaweza ikawa 1) Bwana, ambaye siku zote hutenda haki, atakuja na kuwaponya watu waokatika siku hiyo au 2) katika siku hiyo Bwana atajidhihirisha kwa watu wake wenye haki na kuwaponya.

mbawa

mbawa

Utangulizi wa Injili ya Mathayo

Sehemu ya 1: Utangulizi wa Ujumla

Maelezo ya Kitabu cha Mathayo

  1. Kuzaliwa kwa Yesu Kristo na mwanzo wa huduma yake (1:1-4: 25)
  2. Mahubiri ya Yesu mlimani (5:1-7:28)
  3. Yesu anaonyesha ufalme wa Mungu kupitia matendo ya uponyaji (8:1-9:34)
  4. Mafundisho ya Yesu kuhusu utume na ufalme (9:35-10:42)
  5. Mafundisho ya Yesu kuhusu injili ya ufalme wa Mungu. Mwanzo wa upinzani kwa Yesu. (11:1-12: 50)
  6. Mifano ya Yesu kuhusu ufalme wa Mungu (13:1-52)
  7. Upinzani zaidi kwa Yesu na kutokuelewa kuhusu ufalme wa Mungu (13:53-17:57)
  8. Mafundisho ya Yesu kuhusu uhai katika ufalme wa Mungu (18:1-35)
  9. Yesu ahudumu katika Yudea (19:1-22:46)
  10. Mafundisho ya Yesu kuhusu hukumu ya mwisho na wokovu (23:1-25:46)
  11. Kusulubiwa kwa Yesu, kifo chake na ufufuo wake (26:1-28:19)

Je, kitabu cha Mathayo kinahusu nini?

Injili ya Mathayo ni moja ya vitabu vinne katika Agano Jipya ambavyo vinaelezea kuhusu maisha ya Yesu Kristo. Waandishi wa Injili waliandika juu ya mambo mbalimbali yaliyoonyesha kama Yesu alikuwa nani na ni nini alichofanya. Mathayo aliashiria kwamba Yesu alikuwa Masiya, na kama Mungu angeweza kuokoa Israeli kupitia kwake. Mathayo mara nyingi alielezea kwamba Yesu alitimiza unabii wa Agano la Kale kuhusu Masiya. Hii inaweza kuonyesha kwamba alitarajia kuwa wasomaji wake wengi wa kwanza watakuwa Wayahudi. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#christ)

Je, kichwa cha kitabu hiki kinapaswa kutafsiriwaje?

Watafsiri wanaweza kuchagua kukiita kitabu hiki kwa kichwa chake asilia, "Injili ya Mathayo," au "Injili kulingana na Mathayo." Au wanaweza kuchagua kichwa ambacho ni wazi, kama vile "Habari Njema ya Yesu ambayo Mathayo aliandika." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-names)

Nani aliandika Kitabu cha Mathayo?

Kitabu hakitupi jina la mwandishi. Hata hivyo, tangu nyakati za hapo mwanzo za Kikristo, Wakristo wengi wamefikiri kwamba mwandishi alikuwa Mtume Mathayo.

Sehemu ya 2: Dhana muhimu za Kidini na za Kitamaduni

Je, "Ufalme wa mbinguni" ni nini?

Mathayo alizungumza juu ya ufalme wa mbinguni kwa njia ile ile ambayo waandishi wengine wa injili walizungumzia juu ya Ufalme wa Mungu. Ufalme wa mbinguni unawakilisha Mungu akitawala juu ya watu wote na viumbe vyote kila mahali. Wale ambao Mungu anakubali katika ufalme wake watabarikiwa. Wataishi pamoja na Mungu milele.

Je, njia za kufundisha za kufundisha zilikuwa zipi?

Watu walimwona Yesu kama rabi. Rabi ni mwalimu wa sheria ya Mungu. Yesu alifundisha kwa njia iliyokuwa sawa na njia ya walimu wengine wa kidini huko Israeli. Alikuwa na wanafunzi ambao walimfuata kila mahali alipoenda. Wanafunzi hawa waliitwa wanafunzi. Mara nyingi aliwaambia mifano. Mifano ni hadithi zinazofundisha masomo ya maadili. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lawofmoses and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#disciple na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#parable)

Sehemu ya 3: Masuala muhimu ya Tafsiri

Je, vitabu vya kwanza vya Injili ni vipi?

Vitabu vya Mathayo, Marko na Luka huitwa injili za sinoptiki kwa sababu vina vifungu vingi vinavyofanana. Neno "sinoptiki" linamaanisha "kuona kwa pamoja."

Maandiko husemekana kuwa "sawa" wakati ambapo injili mbili au tatu zinafanana au zinakaribia kufanana. Wakati wa kutafsiri vifungu sambamba, wafasiri wanapaswa kutumia maneno sawa na kuyafananisha iwezekanavyo.

Je, kwa nini Yesu anajiita mwenyewe kama "Mwana wa Binadamu"?

Katika Injili, Yesu anajiita mwenyewe "Mwana wa Binadamu." Ni kumbukumbu ya Danieli 7:13-14. Katika kifungu hiki kuna mtu anayeelezewa kuwa "Mwana wa binadamu." Hiyo ina maana kwamba mtu huyo alifanana na mwanadamu. Mungu alitoa mamlaka kwa mwana wa binadamu kutawala mataifa milele. Na watu wote watamwabudu milele.

Wayahudi wa wakati wa Yesu hawakutumia "Mwana wa Binadamu" kama jina la mtu yeyote. Kwa hiyo, Yesu aliitumia kwa ajili yake mwenyewe ili kuwasaidia kuelewa kama yeye alikuwa nani. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sonofman)

Kutafsiri jina "Mwana wa Binadamu" kunaweza kuwa vigumu kwa lugha nyingi. Labda wasomaji hawataelewa tafsiri halisi. Watafsiri pia wanaweza kutumia jina mbadala, kama vile "Yule aliye Mtu." Inaweza pia kusaidia wanapoingiza maelezo ya chini ya tanbihi ili kulielezea.

Je, ni yapi masuala makuu katika maandishi ya Kitabu cha Mathayo?

Haya ni masuala muhimu zaidi ya maandishi katika Kitabu cha Mathayo:

Watafsiri wanashauriwa kutoingiza vifungu hivi. Hata hivyo, ikiwa katika eneo la watafsiri, kuna matoleo ya zamani ya Biblia ambayo yanajumuisha moja au zaidi ya vifungu hivi, watafsiri wanaweza kuvijumuisha. Ikiwa vinajumuishwa, wanapaswa kuviweka ndani ya mabano ya mraba ([]) ili kuonyesha kwamba labda asili yao sio Injili ya Mathayo. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/jit.html#translate-textvariants)

Matthew 1

Mathayo 01 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri hupendelea kuweka kando kidogo nukuu za Agano la Kale. ULB na tafsiri nyingine nyingi za Kiingereza huingiza mistari ya 1:23, ambayo ni nukuu kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

Nasaba

Nasaba ni orodha ambayo hurekodi mababu au wazao wa mtu. Orodha hizo zilikuwa muhimu sana katika kuamua nani aliyekuwa na haki ya kuwa mfalme, kwa sababu mamlaka ya mfalme mara nyingi ilipokelewa au kurithiwa kutoka kwa baba yake. Ilikuwa pia ya kawaida kwa mtu yeyote mashuhuri kuwa na kizazi cha kumbukumbu.

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Matumizi ya sauti tulivu

Sauti tulivu hutumiwa kwa makusudi katika sura hii ili kuonyesha kwamba Yesu hakuzaliwa kupitia uhusiano wa ngono. Hapa, sauti tulivu inaashiria Roho Mtakatifu kama aliyetanguliza uja uzito wake Maria alipombeba mtoto Yesu. Kwa kuwa lugha nyingi hazina sauti tulivu, watafsiri wanapaswa kutafuta njia nyingine za kuwasilisha ukweli huo. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-activepassive)

| >>

Matthew 1:1

Taarifa kwa ujumla:

Mwandishi anaanza na ukoo wa Yesu ili kuonesha kwamba yeye ni mzaliwa wa mfalme Daudi na wa Ibrahimu.

Kitabu cha ukoo wa Yesu Kristo

Ungeweza kutafsiri hii kama sentenso kamili.

mwana wa Daudi, mwana wa Ibrahimu

Kulikuwa na vizazi vingi kati ya Yesu, Daudi, na Ibrahimu. Hapa "mwana" humaanisha "mzaliwa" "mzaliwa wa Daudi, ambaye alikuwa mzaliwa wa Ibrahimu.

mwana wa Daudi

wakati mwingine kirai "mwana wa Daudi" hutumika kama cheo, lakini hapa inaonekana kutumika kutambulisha tu ukoo wa Yesu.

Ibrahimu alikuwa baba wa Isaka

Kuna njia mbalimbali ungeweza kutafsiri maelezo haya. Kwa namna yoyote unavyo natafsiri hapa, ingekuwa bora zaidi kuyatafsiri kwa namna ilele kwa orodha yote ya mababu wa Yesu. "Ibrahimu akawa baba wa Isaka" au "I brahimu alikuwa na mwana Isaka" au "Ibrahimu alikuwa na mwana aliitwa Isaka."

Peresi na Sera...Hesroni...Ramu

Haya ni majina ya wanaume

Peresi baba... Hesroni baba

"Peresi alikuwa baba... Hesroni alikuwa baba.

Matthew 1:4

Salmoni alikuwa baba wa Boazi kwa Rahabu

"Salamoni alikuwa baba wa Boazi, na mama wa Boazi alikuwa Rahabu" au "Salmoni na Rahabu walikuwa wazazi wa Boazi.

BOazi baba wa Obedi kwa Ruth

"Boazi alikuwa baba wa Obedi, na mama wa Obedi alikuwa Ruth" au "Boazi na Ruth walikuwa wazazi wa Obedi"

Daudi alikuwa baba wa Sulemani kwa mke wa Uria.

"Daudi alikuwa baba wa Sulemani, na mama wa Sulemani alikuwa mke wa Uria" au "Daudi na mke wa Uria walikuwa wazazi wa Sulemani"

mke wa Uria

Sulemani alizaliwa baada ya Uria kufa. "mjane wa Uria."

Matthew 1:7

Yoramu baba wa Uzia

Yoramu alikuwa kwa kweli babu ya babu yake na Uzia, hivyo 'baba" linaweza kutafsiriwa kama " babu"

Matthew 1:9

Amoni

Wakati mwingine jina hili limetafsiriwa "Amosi"

Yosia alikuwa baba wa Yekonia

Yosia alikuwa kwa kweli babu yake na Yekonia.

wakati wa kuchukuliwa kwenda Babeli

"wakati walipoamriwa kwa nguvu kuondoka kwenda Babeli" au "wakati Wababeli walipo washinda na kuwahamisha kwenda kuishi Babeli." Kama lugha yako inahitaji kuwataja wazi ambao walienda Babeli, unaweza kusema "Waisraeli" au Waisraeli ambao waliishi Yuda.

Babeli

Hapa humaanisha nchi ya Babeli, sio tu mji wa Babeli.

Matthew 1:12

baada ya kuchukuliwa kwenda Babeli

Tumia maneno yale yale uliyoyatumia katika Mat.1:9

Shealitieli baba ya Zerubabeli

Shealitieli kwa kweli alikuwa babu yake na Zerubabeli.

Matthew 1:15

Maelezo yanayounganisha

Mwandhishi anahitimisha ukoo wa Yesu, ambayo yalianza katika Mat.1: 1

Mariamu, ambaye kwa yeye Yesu alizaliwa

Mariamu, ambaye alimzaa Yesu

Aitwaye Kristo

Hii inaweza kuelezwa kwa namna iliyo hai. "watu ambao humwita Kristo."

Kumi na nne

"14"

kuchukuliwa kwenda Babeli

Tumia maneno yale yale uliyotumia katika Mat.1:9.

Matthew 1:18

Taarifa kwa ujumla:Mama yake alikuwa amechumbiwa kuolewa na Yusufu

"Mama yake Mariamu alikuwa mbioni kuolewa na Yusufu" kwa kawaida wazazi walifanya mipango ya ndoa za watoto wao." Wazazi wa Mariamu, mama wa Yesu, walikuwa wamemwahidi kuolewa na Yusufu.

Mama yake Mariamu alikuwa amechumbiwa

Tafsiri kwa namna ambayo huweka wazi kwamba Yesu alikuwa bado hajazaliwa wakati Mariamu alikuwa amechumbiwa na Yusufu. "Mariamu, ambaye angekuwa mama wa Yesu, alikuwa amechumbiwa,"

Kabla hawajapata kuwa pamoja

"kabla hawajaoana." Hii pengine inamaanisha Mariamu na Yusufu kulala pamoja. kabla hawajalala pamoja."

alionekana kuwa mjamzito

Hii inaweza kuelezwa kwa namna iliyo tendaji. "wakatambua kwamba alikuwa mbioni kupata mtoto" au 'ilitokea kuwa alikuwa mjamzito.

kwa Roho Mtakatifu

Uwezo wa Roho Mtakatifu ulikuwa umemwezesha kupata mtoto kabla ya kuwa amelala na mwanamume.

Mumewe Yusufu

Yusufu alikuwa bado hajamwoa Mariamu, lakini wakati mwanamume na mwanamke waliahidi kuoana, Wayahudi waliwahesabu mume na mke ingawa hawakuishi pamoja. "Yusufu, ambaye aliyepaswa kumwpoa Mariamu" au "Yusufu."

alisitisha uchumba kati yake na yeye

kuvunja mipango ya kuoana

Matthew 1:20

Kama alivyofikiri

"Kama Daudi alivyofikiri"

alimtokea katika ndoto

"alikuja kwake wakati Yusufu alikuwa akiota ndoto"

mwana wa Daudi

Hapa "mwana" humaanisha "mzaliwa"

aliyechukuliwa mimba katika tumbo lake amechukliwa mimba kwa Roho Mtakatifu

Hii inaweza kuelezewa kwa namna iliyo tendaji. "Roho Mtakatifu alisababisha Mariamu kuwa mjamzito na kuwa na mtoto huyu."

Naye atamzaa mwana

Kwa sababu Mungu alimtuma malaika, malaika alijua mtoto atakuwa mvulana.

utamwita jina lake

Hii ni amri. "utamwita" au "yakupasa kumpa jina"

kwa kuwa ataokoa

Mtafsiri anaweza kuongeza rejeo inayo sema "Jina 'Yesu' maana yake Bwana huokoa."

watu wake

Hii humaanisha Wayahudi

Matthew 1:22

Taarifa kwa ujumla

Mwandishi amnukuu nabii Isaya kuonesha kwamba kuzaliwakwa Yesu kulikuwa kwa mujibu wa andiko

Hii yote ilitokea

Malaika hazungumzi tena. Mathayo sasa anaeleza umuhimu wa kile malaika alikisema.

kilichonenwa na Bwana kwa njia ya nabii

Hii inaweza kuelezwa kwa namna iliyo tendaji. "kile ambacho Bwana alimwambia nabii Isaya kuandika zamani."

Tazama...Emanueli

Hapa Mathayo anamnukuu nabii Isaya.

Tazama

Neno hili huongeza msisitizo kwa kile kilicho fuata kusemwa. "Tazama" au "Sikia" au "Kuwa makini kwa kile ninachotaka kukuambia"

Emanueli

Hili ni jina la kiume.

maana yake 'Mungu pamoja nasi'

Hii haimo katika kitabu cha Isaya. Mathayo anaeleza maana ya jina "Emanueli." Unaweza kulitafsiri kama sentenso iliyo peke yake. "Jina hili maana yake 'Mungu pamoja nasi.'"

Matthew 1:24

Maelezo yanayo unganisha:

Mwandishi anahitimisha maelezo ya matukio kuelekea kuzaliwa kwa Yesu.

kama malaika wa Bwana alivyoamuru

Malaika alikuwa amemwambia Yusufu kumchukua Mariamu kama mke wake na kumpa mtoto jina Yesu.

akamchukua kama mke wake

"alimwoa Mariamu"

kwa mwana

Hakika ni wazi kuwa Yusufu si baba halisi "kwa mtoto wa kiume" au "kwa mwana wake."

Na alimwita jina lake Yesu

"Yusufu alimwita mtoto Yesu"

Matthew 2

Mathayo 02 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri hupendelea kuweka kando kidogo nukuu za Agano la Kale. ULB na tafsiri nyingine nyingi za Kiingereza huingiza mstari yote ya mistari ya 6 na18, ambayo ni nukuu kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

"Nyota yake"

Huenda labda inaelezea nyota ambayo wasomi waliamini kuwa ishara ya mfalme mpya wa Israeli. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sign)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Waakili"

Tafsiri za Kiingereza hutumia maneno mengi tofauti ili kutafsiri maneno haya. Maneno haya ni pamoja na "wanajimu" na "watu wenye hekima." Watu hawa wangeweza kuwa wanasayansi au majusi. Ni bora kutafsiri hii kwa neno la kawaida "waakili," inapowezekana.

<< | >>

Matthew 2:1

Taarifa kwa ujumla:

Sehsmu mpya ya habari huanza hapa na kuendelea hadi mwisho wa sura. Mwandishi anasimulia kuhusu jaribio la Herode kumwua mfalme mpya wa Wayahudi.

Bthlehemu ya Yuda

"mji wa Bethlehemu katika jimbo la Uyahudi"

katika siku za mfalme Herode

"wakati Herode alipokuwa mfalme huko"

Herode

Hii humaanisha Herode Mkuu.

mamajusi

"watu wenye elimu ya nyota"

kutoka mashariki

"kutoka nchi ya mbali mashariki ya Uyahudi.

Yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi?

Watu wale walijua kutokana na elimu ya nyota kwamba yule ambaye atakuja kuwa mfalme alikuwa amekwisha zaliwa. Walikuwa wanajaribu kuchunguza mahali alipokuwa. Mtoto mdogo ambaye atakuja kuwa mfalme wa Wayahudi amezaliwa. Yuko wapi?"

nyota yake

Walikuwa hawasemi kwamba mtoto mdogo alikuwa mmiliki halali wa nyota. "nyota ambayo hutuambia kuhusu yeye" au "nyota ambayo imehusishwa na kuzaliwa kwake.'

mashariki

"ilikuja tokea mashariki" au wakati tulopkuwa katika nchi yetu"

abudu

uwezekano wa maana ni 1) walikusudia kumwabudu mtoto mdogo kama Mungu, au 2) walitka kumpa heshima kama mfalme wa kibinadamu. Kama lugha yako ina neno ambalo huhusisha maana zote mbili, unapaswa kuzingatia kulitumia hapa.

alifadhaika

"alitaabishwa." Herode alitaabishwa kwamba mtoto mdogo huyu atachukua nafasi yake kama mfalme.

Yerusalemu yote

Hapa "Yerusalemu" ina maanisha watu. Pia "yote" humaanisha "wengi." Mathayo anaongeza chumvi kusisitiza watu wangapi walitaabishwa. "watu wengi wa Yerusalemu."

Matthew 2:4

Taarifa kwa ujumla:

Ktoka mstari wa 6, makuhani wakuu na waandishi wa watu wanamnukuu nabii Mika kuonesha kwamba Kristo angezaliwa Bethlehemu.

Katika Bethlehemu ya Yuda

"Katika mji wa Behlehemu katika jimbo la Yuda"

hili ndilo lililoandikwa na nabii

Hili linaweza kuelezwa kwa namna iliyo tendaji. hiki ndicho likchoandikwa na nabii zamani.

Na wewe, Bethlehemu...Israeli

Wanamnukuu nabii Mika.

wewe, Bethlehemu...hu mdogo miongoni mwa viongozi wa Yuda

MIka alikuwa akizungumza na watu wa Bethlehemu kana kwamba walikuwa pamoja naye, lakini hawakuwa naye. Pia "hu mdogo" linaweza kutafsiriwa na kirai chanya. "ninyi watu wa Bethlehemu,...mji wenu ni miongoni mwa miji iliyo muhimu zaidi kuliko yote katika Yuda.

ambaye atawachunga watu wangu Israeli

Mika anamzungumza mtawala huyu mchungaji. Hii inamaanisha ata waongoza na kuwahudumia watu. "ambaye atawaongoza watu wangu Israeli kama mchungaji aongozavyo kondoo wake."

Matthew 2:7

Herode aliwaita mamajusi kwa siri

Hii inamaanisha kwamba Herode alizungumza na mamajusi bila ya watu wengine kujua.

kuwauliza lini hasa nyota ilikuwa imekwisha onekana.

Hii inaweza kutafsiriwa kama nukuu ya moja kwa moja. "na akawauliza, lini hasa nyota hii ilionekana?"

nyota ilikuwa imeonekana lini

Hii inadokeza kwamba mamajusi walimwambia nyota ilionekana lini. "wakati gani nyota ilikuwa umeonekana. Mamajusi walimwambia Herode lini wakati nyota ilipoonekana mara ya kwanza."

mtoto mchanga

Inamaanisha Yesu.

nipe neno

"nijulishe" au "niambie"

mwabudu

Tafsiri hii kama ulivyofanya katika Mat 2:1

Matthew 2:9

baada ya

"baada ya mamajusi"

walikuwa wamekwisha iona mashariki

"walikuwa wamekwisha iona ikija kutoka mashariki" au "walikuwa wamekwisha iona katika nchi yao."

ikawatangulia

"iliwaonesha njia" au "iliwaongoza"

ilitulia juu ya

"ilisimama juu"

mahali alipokuwa mtoto

"mahali ambapo mtoto mchanga alikuwapo"

Matthew 2:11

Maelezo yanayounganisha:

Hapa mandhari yanahamia kwenye nyumba mahari Mariamu, Yusufu, na mtoto mchanga Yesu walikuwa wakiishi.

walienda

"Mamajusi walienda"

abudu

Trafsiri neno hili kama ulivyofanya katika Mat.1:1

Hazina zao

"hazina" humaanisha kasha au mifuko waliotumia kubebea hazina. "vyombo ambavyo vilishikilia hazina zao."

Mungu aliwaonya

"Baadaye, Mungu aliwaonya mamajusi." Mungu alijua kwamba Herode alitaka kumdhuru mtoto.

wasirudi kwa Herode

Hii inaweza kutafsiriwa kama nukuu ya moja kwa moja. "kusema, 'Msirudi kwa mfalme Herode."

Matthew 2:13

Taarifa za jumla:

Katika mstari wa 15, mwandishi amnukuu nabii Hosea kuonesha kwamba Kristo angekaa Misri.

walikuwa wameondoka

:mamajusi walikuwa wameondoka"

alimtokea yusufu katika ndoto.

"alikuja kwa Yusufu wakati alipokuwa anaota.

Amka, chukua...kimbilia...Baki...wewe

Mungu anazungumza na Yusufu, haya yanapaswa kuwa katika umoja.

hadi nitakapo kuambia

Maana kamili ya maelezo haya yanaweza kufanywa kuwa wazi. "mpaka nitakapo kuambia ni salama kurudi."

Nita kuambia

Hapa "nitakapo kuambia" inamaanisha Mungu. Malaika anazungumza kwa ajili ya Mungu.

Alibaki

Inamaanisha kwamba Yusufu, Mariamu, na Yesu walibaki Misri. "Walibaki"

mpaka kifo cha Herode

Herode hafi mpaka Maelezo haya yanaelezea urefu wa muda wa kukaa Mirsi, na hayasemi kwamba Herode alikufa kwa wakati huu.

Kutoka Misri nitamwita mwanangu

"Nimemwita mwanangu kutoka Misri"

Matthew 2:16

Maelezo yanayounganisha:

Hapa mandhari yahamia kurudi kwa Herode na hueleza alifanya nini baada ya kugundua kuwa mamajusi walikuwa wamemdanganya.

Taarifa kwa ujumla

Matukio haya yalitokea kabla kifo cha Herode, ambayo mwandishi ameyataja katika2:13

amekwisha dhihakiwa na mamajusi

Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "mamajusi walikuwa wamemwaibisha kwa kumdanganya."

Alituma na kuwaua watoto wote wa kiume

Herode hakuua watoto yeye mwenyewe. "Alitoa amri ili maaskali wake watoto wote wa kiume" au "Aliwatuma maaskari pale kuwa watoto wote wa kiume.

wenye umri wa miaka miwili na chini yake

"Umri wa miaka 2 na wadogo chini ya umri huo.

kwa mujibu wa wakati

"kutegemeana na wakati"

Matthew 2:17

Taarifa kwa ujumla:

Mwandishi amnukuu nabii Yeremia kuonesha kwamba kifo cha watoto wote wa kiume katika mkoa wa Bethlehemu kilikuwa kwa mujibu wa Maandiko.

Kisha ilitimizwa

Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "Hii ilitimizwa" au "matendo ya Herode yalitimiza."

kile kilicho kuwa kimenenwa kwa njia ya nabii Yeremia

Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "kile Bwana alikinena hapo zamani kwa njia ya nabii Yeremia"

Sauti ilisikika...hawakuwapo

Mathayo anamnukuu nabii Yeremia.

Sauti ilisikika

Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "Watu walisikia sauti" au "kulikuwa na sauti kubwa."

Raheli awalilia watoto wake

Raheli aliishi miaka mingi kabla ya wakati huu. Unabii huu huonesha Raheli, ambaye amekufa, akiwalilia wazaliwa wake.

alikataa kufarijiwa

Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "hakuna yeyote angeweza kumfariji"

kwa sababu hawapo tena

kwa sababu watoto walikuwa wametoweka na kamwe hawatarudi." Hapa "hawapo tena" ni njia laini ya kusema wamekufa. "kwa sababu walikuwa wamekufa"

Matthew 2:19

Maelezo yanayounganisha:

Hapa mandhari ya hamia kwenda Misri, mahali Ysufu, Mariamu, na mtoto Yesu wanaishi.

tazama

Hii inaweka alama ya mwanzo wa tukio jingine katika habari ndefu. inaweza kuhusisha watu wengi kuliko matukio yaliyotangulia. Lugha yako inaweza kuwa namna ya kufanya hivi.

wale ambao walitafuta uhai wa mtoto

"wale ambao walikuwa wanamtafuta mtoto ili wamwue"

wale ambao walitafuta

Hii ina maanisha mfalme Herode na washauri wake.

Matthew 2:22

Maelezo yanayounganisha:

Huu ni mwisho wa sehemu ya simulizi ambayo ilianza katika Mat. 2:1. kuhusu jaribio la Herode kumwua mfalme mpya wa Wayahudi.

Lakini aliposikia

"Lakini Yusufu aliposikia"

Arikeleu

Hili ni jina la mwana wa Herode.

aliogopa

"Yusufu aliogopa"

lile lililonenwa na Bwana kwa njia ya nabii

Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "lile Bwana alilolinena hapo zamani kwa njia ya manabii"

ataitwa mnazarayo

Hapa "ataitwa" anamaanisha Yesu. Manabii kabla ya wakati wa Yesu wangelimtaja kama Masihi au Kristo. "watu wangesema kuwa Kristo ni Mnazarayo."

Matthew 3

athayo 03 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri hupendelea kuweka kando kidogo nukuu za Agano la Kale. ULB na tafsiri nyingine nyingi za Kiingereza huingiza mistari yote ya mstari wa 3, ambayo ni nukuu kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

"Zaeni matunda yanayostahili toba"

Matunda ni taswira ya kawaida katika maandiko. Inatumika kuelezea matokeo ya tabia nzuri au mbaya. Katika sura hii, matunda mazuri ni matokeo ya kuishi kama Mungu anavyoamuru. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#fruit)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Ufalme wa mbinguni umekaribia"

Wataalam wanajadili ikiwa "ufalme wa mbinguni" ulikuwepo wakati huu au bado unakuja. Tafsiri za Kiingereza mara nyingi hutumia maneno "karibu," lakini hii inaweza kusababisha changamoto katika kutafsiri. Matoleo mengine hutumia maneno "inakaribia" na "yamekaribia."

<< | >>

Matthew 3:1

Taarifa kwa ujumla:

Huu ni mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi mahali ambapo mwandishi anaisimulia huduma ya Yohana Mbatizaji. Katika mst. 3. mwandishi anamnukuu nabii Isaya kuonesha kwamba Yohana Mbatizaji alikuwa mjumbe aliyechaguliwa na Mungu kuandaa huduma ya Yesu.

Katika siku hizo

Hii ni miaka mingi baada ya Yusufuna familia kuondoka Misri na kwenda Nazareti.Hii pengine karibu na wakati ambao Yesu alianza huduma yake. "Baadaye" au "Miaka kadhaa baadaye."

Tubuni

Hii iko katika wingi. Yohana anazungumza na umati.

ufalme wa mbinguni umekaribia

Kirai "ufalme wa mbinguni" humaanisha Mungu kutawala kama mfalme. Kirai hiki kiko katika kitabu cha Mathayo tu. Kama inawezekana, tumia neno "mbinguni" katika tafsiri yako. "Mungu wetu uliye mbinguni baada ya muda mfupi atajionesha mwenyewe kuwa mfalme."

Kwa kuwa huyu ndiye aliyenenwa na nabii Isaya akisema

Hii inaweza kuelezwa katika nmna iliyo tendaji. "Kwa kuwa Isaya nabii alikuwa anamnena Yohana Mbatizaji wakati aliposema."

Sauti ya mtu

Hapa "sauti" humaanisha nafsi yote. "Kuna mtu."

Tengenezeni njia ya Bwana, nyosheni njia yake

"Andaeni njia ya Bwana, nyosheni njia yake." Hii ni sitiari ya ujumbe wa Yohana ambao unawita watu kujiandaa na ujio wa Yesu kwa kufanya toba ya dhambi zao. "Badilika katika maisha yako hivyo utakuwa tayari wakati Bwana ajapo."

Matthew 3:4

Sasa...asali ya nyikani

Neno "sasa" limetumika hapa kuweka alama kutenganisha mtiririko mkuu wa simulizi. Hapa Mathayo ana simulia habari za historia ya nyuma kuhusu Yohana Mbatizaji.

alivaa nguoa za manyoa ya ngamia na mkanda wa ngozi katika kiuno chake.

Vazi hili huashiria kwamba Yohana ni nabii kama manabii wa tangu zamani, hususan nabii Eliya.

Kisha Yerusalemu, Uyahudi yote, na mkoa wote

Hii humaanisha watu kutoka maeneo yale. "Hapa neno "yote" humaanisha "wengi." Mathayo anasisitiza jinsi watu wengi walivyoenda kwa Yohana Mbatizaji.

Walibatizwa naye

Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "Yohana aliwabatiza."

Wao

Hii inamaanisha watu waliokuja kutoka Yerusalemu, Uyahudi, na mkoa kuzunguka Mto Yordani.

Matthew 3:7

Taarifa kwa ujumla:

Yohana Mbatizaji aanza kuwakemea Mafarisayo na Masadukayo.

Enyi uzao wa nyoka wa sumu

Hii ni sitiari. Nyoka wa sumu ni hatari na wanwaklisha uovu. "Enyi nyoka wa sumu waovu!" au "Mu waovu kama nyoka wa sumu."

nani kawaonya kuikimbia ghadhabu ambayo inakuja

Yohana anatumia swali kuwaonya Mafarisayo na Masadukayo kwa sababu walikuwa wakimwomba kuwabatiza ili kwamba Mungu asiwahukumu, lakini hawakutaka kuacha kufanys dhambi. "hamwezi kuikimbia ghadhabu ya Mungu namna hii" au "msifikiri kwamba mnaweza kuikimbia ghadhabu ya Mungu kwa sababu ya kuwabatiza tu.

Ikimbieni gadhabu inayokuja

Neno "ghadhabu" linatumika kumaanisha adhabu ya Mungu kwa sababu ghadhabu yake hutangulia. "kimbieni kutoka kwenye hukumu ambayo inakuja" au "iepukeni kwa sababu Mungu anaenda kuwaadhibu ninyi."

Zaeni matunda yastahiliyo toba

Kirai "zaeni matunda" ni sitiari inayomaanisha matendo ya mtu. "Acha matendo yenu yaoneshe kwamba mmetubu kweli."

Tunaye Ibrahimu baba yetu

"Ibrahimu ni babu yetu" au "ni wazaliwa wa Ibrahimu." Viongozi wa Kiyahudi walifikiri kwamba Mungu hangewahukumu kwa kuwa ni wazaliwa wa Ibrahimu.

Kwa maana nawambieni

Hii inaongeza msisitizo kwa kile Yohana anchokwenda kukisema

Mungu anaweza kumwinulia Ibrahimu watoto hata kutokana na mawe haya.

"Mungu angeweza kufanya wazaliwa wa mwili kutokana hata na mawe haya na kumpa Ibrahimu"

Matthew 3:10

Maelezo yanyounganisha

Yohana Mbatizaji anaendelea kuwakemea Mafarisyo na Masadukayo.

Tayari shoka limekwisha wekwa kwenye shina la miti. Hivyo kila mti usioweza kuzaa matunda mazuri unakatwa na kutupiwa motoni.

Sitiari hii inamaanisha Mungu yuko tayari kuawaadhibu wenye dhambi. Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "Mungu ana shoka lake na yuko tayari kukata na kuchoma mti wowote unaozaa matunda mabaya" au "Kama vile mtu atayarishavyo shoka kukata na kuchoma mti ambao huzaa matunda mabaya, Mungu yuko tayari kuwaadhibu ninyi kwa ajili ya dhambi zenu."

kwa ajili ya toba

"kuonesha kwmba umekwisha tubu"

Lakini ajaye nyuma yangu

Yesu ni mtu yule ambaye anakuja nyuma ya Yohana

ni mwenye uwezo kuliko mimi

'ni wa muhimu zaidi kuliko mimi"

Atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto

Sitiari hii hulinganisha ubatizo wa Yohana wa maji kwa ubatizo ujao wa moto. Hii humaanisha ubatizo wa Yohana kiishara huwatakasa watu dhambi zao. Ubatizo kwa Roho Mtakatifu na moto utatakasa dhambi za watu kwa kweli. Kama inawezekana, tumia neno "batiza" katika tafsiri yenu kutunza ulinganishaji wa ubatizo wa Yohana.

Pepeto lake li mkononi mwake kupepeta ngano

Sitiari hii hulinganisha namna Kristo atakavyo watenganisha watu wenye haki na watu wasio haki kwa namna mtu atenganishavyo nafaka ya ngano na makapi. "Kristo ni kama mtu ambaye pepeto lake liko mkononi mwake."

Pepeto lake li mkononi mwake

Hapa "mkononi mwake" humaanisha mtu yuko tayari kutenda. "Kristo ameshikilia pepeto kwa sababu yuko tayari."

pepeto

Hiki ni kifaa kwa ajili ya kurusha juu hewani kutenganisha nafaka za ngano na makapi. Nafaka zenye uzito hurudi na kuanguka chini na makapi yasiyotakiwa hupeperushwa na upepo. Kina fanana na umbo la uma ya nyasi lakini kina meno mapana kimetengenzwa kutokana na mbao.

sakafu yake ya kupuria

"kiwanja chake" au " kiwanja mahali ambapo hutenganisha nafaka na makapi"

kukusanya ngano yake katika ghala...kuchoma makapi kwa moto usioweza kuzimika

Hii ni sitiari inayoonesha jinsi Mungu atakavyowatenganisha watu wenye haki na watu waovu. Wenye haki wataenda mbinguni kama ngano katika ghala ya mkulima, na Mungu atawachoma watu ambao ni kama makapi kwa moto ambao hautazimika.

hautaweza kamwe kuzimika

Hii inweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "kamwe hautazimika."

Matthew 3:13

Maelezo yanayounganisha

Hapa mandhari yahamia kwenda wakati wa baadaye wakati Yohana Mbatizaji ambatiza Yesu.

kubatizwa na Yohana

Hii inaweza kueleza katika namna iliyo tendaji. "hivyo Yohana aliweza kumbatiza."

Nina hitaji kubatizwa wewe, nawe waja kwangu?

Yohana anatumia swali kuonesha kushangazwa kwake na ombi la Yesu. "Wewe ni wa maana zaidi kuliko mimi. Sipaswi kukubatiza wewe. Wewe unapaswa kunibatiza mimi."

kwa ajili yetu

Hapa "sisi" humaanisha Yesu na Yohana.

Matthew 3:16

Maelezo yanayounganisha

Huu ni mwisho wa sehemu ya simulizi kuhusu Yohana Mbatizaji na hueleza kilichotokea baada ya kumbatiza Yesu.

Baada ya kubatizwa

Hii inaweza kueleza katika namna iliyo tendaji. "Baadaya Yohana kumbatiza Yesu"

tazama

Neneo "tazama" hapa hututahadharisha sisi kuwa makini kwa habari ya kushtukiza ambayo inafuata.

mbingu zilifunguka kwake

Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "Yesu aliona mbingu zimefunguka" au "Mungu alizifungua mbingu kwa Yesu."

kushuka chini kama njiwa

Maana zinaweza kuwa 1) haya ni maelezo dhahiri kwamba Roho alikuwa katika umbo la njiwa au 2) huu ni mfanano ambao hulinganisha Roho kushuka chini kuja juu ya Yesu kwa upole, ndivyo njiwa angefanya.

sauti toka ilitoka mbinguni ikisema

"Yesu alisikia sauti kutoka mbinguni." Hapa "sauti" humaanisha Mungu anazungumza. "Mungu alizungumza kutoka mbinguni."

Mwana

Hiki ni cheo cha maana cha Yesu, Mwana wa Mungu

Matthew 4

Mathayo 04 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri hupendelea kuweka kando kidogo nukuu za Agano la Kale. ULB na tafsiri nyingine nyingi za Kiingereza huingiza mistari yote ya mistari ya 6, 10, 15 na 16, ambayo ni nukuu kutoka Agano la Kale.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Ufalme wa mbinguni umekaribia

Wataalam wanajadili ikiwa "ufalme wa mbinguni" ulikuwepo wakati huu au bado unakuja. Tafsiri za Kiingereza mara nyingi hutumia maneno "karibu," lakini hii inaweza kusababisha changamoto katika kutafsiri. Matoleo mengine hutumia maneno "inakaribia" na "yamekaribia."

"Ikiwa wewe ni Mwana wa Mungu"

Kwa Kiingereza, msomaji anaweza kuelewa kauli hii katika 4:6 kama inayoonyesha kwamba Shetani hajui kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu. Kwa sababu Shetani anajua kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, haipaswi kutafsiriwa kwa njia hii. Inaweza kutafsiriwa kama "kwa sababu wewe ni Mwana wa Mungu." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#satan na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sonofgod)

<< | >>

Matthew 4:1

Taarifa kwa ujula:

Hapa mwandishi anaanza sehemu mpya ya simulizi ambayo Yesu anatumia siku 40 nyikani, mahali ambapo Shetani anamjaribu. Katika mst. 4, Yesu anamkemea Shetani kwa nukuu kutoka Kumbukumbu la Torati.

Yesu aliongozwa na Roho

Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "Roho alimwongoza Yesu."

kujaribiwa na Ibilisi

Hiiinaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "hivyo Ibilisi aliweza kumjaribu Yesu."

Ibilisi...Mjaribu

Haya yana maanisha kiumbe yuleyule. unaweza kutumia neno lilelile kutafsiri yote mawili.

alikuwa amefunga ...alikuwa na njaa

Haya yanamaanisha Yesu.

siku arobaini mchana na usiku

"Siku 40 mchana na usiku" Hii ina maanisha vipndi vya saa 24. "siku 40."

Kama wewe ni mwana wa Mungu, amuru

Ina wezekana kuwa na maana 1) hili ni jaribu la kufanya miujiza kwa ajili ya manufaa ya Yesu mwenyewe. "Wewe ni mwana wa Mungu, hivyo amuru." Au 2) "Thibitisha kwamba wewe ni Mwana wa Mungu kwa kuamuru." Ni vizuri kuamini kuwa Shetani alijua kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu.

Mwana wa Mungu

Hiki ni cheo muhimu kinacho eleza uhusiano kati ya Yesu na Mungu.

Mwana wa Mungu

Hikini cheo cha maana cha Yesu.

amuru mawe haya kuwa mkate

Ungeweza kutafsiri hii na nukuu ya moja kwa moja. "sema kwa mawe haya, Kuwa mkate."'

mkate

"chakula"

imeandikwa

Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "Musa aliandika hivi katika maandiko hapo zamani."

Mtu hataishi kwa mkate tu

Hii inamaanisha kuwa kuna kitu ambacho ni cha muhimu zaidi katika maisha kuliko chakula

bali kwa kila neno ambalo hutoka katika kinywa cha Mungu.

Hapa "neno" na "kinywa" humaanisha kwa kile Mungu anasema.

Matthew 4:5

Taarifa za Jumla:

Katika mstari 6, Shetani ananukuu kutoka Zaburi ili kumjaribu Yesu.

Kama wewe ni Mwana wa Mungu, jitupe chini

Inaweza kuwa na maana 1) hili ni jaribu kufanya muujiza kwa ajili ya manufaa ya Yesu mwenyewe. "Kwa kuwa Mwana wa Mungu kwa kweli, unaweza kujitupa chini." Au, 2) hii ni changamoto au shtaka. "Thibitisha kuwa wewe kwakweli ni Mwana wa Mungu kwa kujitupa chini" Ni vizuri kuamini kuwa Shetani alijua kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu.

Mwana wa Mungu

Hiki ni cheo cha maana ambacho kinaeleza uhusiano kati ya Mungu na Yesu.

jitupe chini

"jiachie mwenyewe hadi chini" au ruka kwenda chini"

kwa maana imeandikwa

Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "kwa maana mwimba zaburi aliandika katika maandiko" au " kwa maana inasema katika maandiko."

Ataagiza malaika wake wakutunze

"Mungu atawaagiza malaika wake wakutunze." Hii inaweza kutafsiriwa na nukuuu ya moja kwa moja. "Mungu atasema kwa malaika wake, Mlindeni."'

Watakuinua juu

"Malaika watakushika

Matthew 4:7

Taarifa kwa ujumla:

Katika mstari wa 7, Yesu amemkemea Shetani na nukuu nyingine kutoka Kumbu kumbu

Tena imeandikwa

Imefahamika kuwa Yesu anamaanisha ana nukuu maandiko tena. Hii inaweza kuelezwa katika namna iliyo tendaji. "Tena, nitawaambia Musa alichoandika katika maandiko."

Usimjaribu

Hapa "usi" inamaanisha yeyote. "Mtu hapaswi kumjaribu" au "Hapana mtu anapaswa kumjaribu."

Tena, Ibilisi

"Baada ya hapo, Ibilisi"

Alimwambia

"Ibilisi alimwambia Yesu"

Vitu vyote hivi nitakupa

"Nitakupa vitu vyote hivi." Mjaribu anasisitiza kuwa atampa "vitu vyote," si tu baadhi yake.

Matthew 4:10

Maelezo yanayounganisha:

Huu ni mwisho wa sehemu ya simulizi kuhusu jinsi Shetani alivyo mjaribu Yesu

Taarifa kwa ujumla

Katika mstari su10, Yesu anamkemea ShetanTi na nukuu nyingine kutoka Kumbukumbu la Torati.

Kwa maana imeandikwa

Hii inaweza kuelezwa katika namna yamuundo tendaji. "Musa pia aliandika katika maandiko."

Yakupasa

Hapa "yakupasa" inamaanisha yeyote.

Tazama

Neno "tazama" hapa lina tutahadharisha kuwa makini kwenye habari mpya muhimu ambazo zinafuata.

Matthew 4:12

Taarifa kwa ujumla:

Huu ni mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi ambayo katika hiyo mwandishi anaeleza mwanzo wa huduma ya Yesu Galilya. Mistari hii inaeleza jinsi Yesu alivyokuja Galilaya

Sasa

Neno hili lintumika hapa kuweka alama ya kuanzisha mtiririko wa habari kuu wa simulizi. Hapa Mathayo anaanza kutuambia sehemu mpya ya simulizi.

Yohana alikuwa amekamatwa

Hii inaweza kuelezwa katika namna ya muundo tendaji. "mfalme alikuwa amemkamata Yohana."

Katika majimbo ya Zabuloni na Naftali

Haya ni majina ya makabila ambayo yaliishi katika maeneo haya kabla ya wageni kudhibiti nchi ya Israeli miaka mingi kabla.

Matthew 4:14

Taarifa kwa ujumla:

Katika mstari wa 15 na 16, mwandishi anamnukuu nabii Isaya kuonesha kwamba huduma ya Yesu Galilaya ilikuwa ni kutimizwa kwa unabii.

Hii ilitokea

Hii inamaanisha Yesu kwenda kuishi Kaperenaumu.

kilichonenwa

Hii inaweza kuelezwa katika namna ya muundo tendaji. "kile Mungu alichonena"

Nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali...Galilaya ya Wamataifa.

Majimbo haya yote yanaeleza eneo lilelile. Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi timilifu. "Katika jimbo la Zabuloni na Naftali...katika jimbo hilo huishi Wamataifa wengi."

kuelekea bahari

Hii ni bahari ya Galilaya.

Watu waliokaa katika giza wameona mwanga mkuu

Hapa "giza" humaanisha maisha ya gizani au dhambi ambayo huwatenga watu na Mungu. Na "mwanga" humaanisha ujumbe wa kweli wa Mungu ambao huwaokoa watu kutoka katika dhambi yao. Hii ni taswira ya watu ambao hawa kuwa na tumaini sasa wana tumaini kutoka kwa Mungu.

kwa hao ambao walikaa katika eneo na kivuli cha kifo, juu yao mwanga umewazukia

Kimsingi hii ina maana ileile kama sehemu ya kwanza ya sentensi. Hapa "eneo" na kivuli cha kifo" humaanisha kifo cha kiroho au kutengana na Mungu.

Matthew 4:17

Tubuni, kwa kuwa ufalme wa mbinguni umekaribia

Sentensi "ufalme wa mbinguni" humaanisha utawala ambao Mungu ndiye mfalme. Sentensi hii imetumika katika injili ya Mathayo tu. Kama inawezekana tumia neno "Mbinguni" katika tafsiri yako. "Si muda mrefu Baba yetu aliye mbinguni atajidhirisha kuwa ni mfalme" Angalia jinsi ilivyotafsiriwa katika Mat. 3:1

Matthew 4:18

Taarifa za jumla:

Hii huanza mandhari mpya katika sehemu ya simulizi kuhusu huduma ya Yesu kule Galilaya. Hapa huanza kwa kuwakusanya watu kuwa wanafunzi wake.

Kutupa nyavu baharini

"Kutupa nyavu majini ili kuvua samaki"

Nifuateni

"Yesu anawakaribisha Simoni na Andrea kumfuata, kuishi naye, na kuwa wanafunzi wake. ""Iweni wanafunzi wangu."

Nitawafanya wavuvi wa watu

Hii sitiari humaanisha Simoni na Andrea watawafundisha watu ujumbe wa kweli wa Mungu hivyo wengine pia waanze kumfuata Yesu. "Nitawafundisha kuwaleta watu kwangu kama mlivyo kuwa mnavua samaki"

Matthew 4:21

Sentensi unganishi

Yesu anawaita watu zaidi kuwa wanafunzi wake.

Aliwaita

"Yesu aliwaita Yohana na Yakobo." Kirai hiki pia humaanisha kwamba aliwakaribisha kumfuata, kuishi naye, na kuwa wanafunzi wake.

maramoja

"wakati huo huo"

waliuacha mtumbwi...na walimfuata

Inapaswa kuwa wazi kwamba haya ni mabadiliko ya maisha. Watu hawa hawaendi tena kuwa wavuvi na wanaacha shughuli za familia zao kumfuata Yesu kwa maisha yao waliyo nayo.

Matthew 4:23

Sentensi unganishi

Huu ni mwisho wa sehemu ya simulizi kuhusu mwanzo wa huduma ya Yesu Galilaya. Mistari hii ni muhtasari wa kile alichofanya na jinsi watu walivyoitikia.

kufundisha katika masinagogi yao

"kufundisha katika masinagogi ya Wagalilaya" au kufundisha katika masinagogi ya watu wale"

kuhubiri injili ya ufalme

Hapa "ufalme" humaanisha utawala wa Mungu kama mfalme. "kuhubiri habari njema kuhusu jinsi Mungu atakavyojifunua mwenyewe kama mfalme."

"aina zote za maradhi na aina zote za magonjwa"

"kila maradhi na kila ugonjwa." Maneno "maradhi" na :magonjwa" yanakaribia sana lakini yanapaswa kutafsiriwa kama maneno mawili tofauti kama inawezekana. "Maradhi ni kile kinacho sababisha mtu kuwa mgonjwa. "Ugonjwa ni udhifu wa mwili au maumivu ambayo ni matokeo ya kuwa na maradhi.

wale waliopagawa na pepo

Hii inaweza kuelezwa katika namna ya mfumo tendaji. "walio na pepo" au "wale ambao wanatawaliwa na pepo."

wenye kifafa

"wale waliokuwa na kifafa" au wale walio na maradhi ambayo yalisababisha kuzirai."

waliopooza

"wale ambao hawakuweza kutembea"

Dekapoli

Jina hili humaanisha "Miji Kumi."

Matthew 5

Mathayo 05 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Mathayo 5-7, ambayo huitwa "Mahubiri ya Mlimani," ni funzo moja ndefu ya Yesu. Mgawanyiko wa sura husababisha kuchanganyikiwa hapa. Kichwa kinaweza kumsaidia msomaji kuelewa kwamba sura hizi zinaunda sehemu moja au kitengo. Mtafsiri anapaswa kufahamu kuwa kuna swali fulani kuhusu ikiwa mafundisho yanahusu Israeli, kanisa, au ufalme wa Mungu wa baadaye.

5:3-10, inayojulikana kama Heri au Baraka, imewekwa kwa kutumia uingizaji, na kila mstari unaanza na neno "heri." Uingizaji huu unaashiria fomu ya ushairi wa mafundisho haya.

Dhana maalum katika sura hii

"Wanafunzi wake"

Inawezekana kutaja mtu yeyote aliyemfuata Yesu kama mfuasi au mwanafunzi. Yesu aliwachagua wafuasi wake kumi na wawili kuwa watu wake wa ndani, wale wanafunzi kumi na wawili. Baadaye walijulikana kama mitume. Inaweza kuwa na maana kwamba mafundisho haya yalikuwa kwa mitume hao kumi na wawili.

<< | >>

Matthew 5:1

Sentensi unganishi

Huu ni mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi ambayo Yesu alianza kuwafundisha wanafunzi wake. Sehemu hii huendelea hadi mwisho wa sura ya 7 na mara kwa mara huitwa mahubiri ya Mlimani.

Maelezo ya jumla

Katika msyari wa 3, Yesu anaanza kueleza tabia za watu ambao wamebarikiwa.

Akafunua kinywa chake

"Yesu alianza kunena."

aliwafundisha

Neno "aliwa" humaanisha wanafunzi wake.

maskini katika roho

Hii inamaanisha mtu ambaye ni mnyenyekevu. "wale ambao wanajua wanamhitaji Mungu."

Kwa kuwa uflmeme wa mbinguni ni wao

Hapa "ufalme wa mbinguni" humaanisha utawala wa Mungu kama mfalme. Kirai hiki kiko katika kitabu cha Mathayo tu. Kama inawezekana weka "mbinguni" katika tafsiri yako. "kwa kuwa Mungu wa mbinguni atakuwa mfalme wao."

wale ambao wana huzunika

Sababu zinazopelekea kuwa wenye huzuni ni 1) hali ya dhambi ya ulimwengu au 2) dhambi zao au 3) kifo cha mtu. Usieleze bayana sababu ya kuhuzunika isipkuwa lugha yako inataka hivyo.

watafarijiwa

Hii inaweza kuelezwa katika namna ya mfumo tendaji. "Mungu atawafariji."

Matthew 5:5

wanyenyekevu

"wapole" au "wale ambao hawategemei uwezo wao wenyewe"

watarithi nchi

"Mungu atawapa nchi yote."

wenye njaa na kiu ya haki

Sitiari hii humaanisha mtu anapaswa kwa uhodari kufanya kilicho sahihi. "kutamani kuishi kwa unyofu kama ilivyo kutamani chakula na kinywaji.

watashibishwa

Hii inaweza kuelezwa katika namna ya mfumo tendaji. "Mungu atawashibisha" au "Mungu atawatosheleza."

walio safi wa moyo

"watu ambao mioyo yao ni safi." Hapa "safi" hurejelea kwa kutamani kwa mtu. wale ambao tu wanataka kumtumikia Mungu."

watamwona Mungu

Hapa "kuona" inamaanistha wataweza kuishi katika uwepo wa Mungu." "Mungu atawaruhusu kuishi naye."

Matthew 5:9

wapatanishi

Hawa ni watu ambao husaidia wengine kuwa na amani na wengine miongoni mwao.

kwa kuwa wataitwa wana wa Mungu

Hii inaweza kuelezwa katika namna ya muundo tendaji. "kwa kuwa Mungu atawaita watoto wake" au "watakuwa watoto wa Mungu.

wana wa Mungu

Ni vizuri kutafsiri "wana" kwa neno lile lile lugha yako kwa kawaida ungelitumia kurujelea kwa mwana au mtoto wa binadamu

wale ambao wameteswa

Hii inaweza kuelezwa katika namna muundo tendaji. "watu wale ambao wengine huwatendea kwa isivyo haki"

kwa ajili ya haki

"kwa sababu wanafanya kile ambacho Mungu hutaka wafanye"

ufalme wa mbinguni ni wao

angalia jinsi ulivyotafsiri katika Mat. 5:1

Matthew 5:11

Sentensi unganishi

Yesu anamaliza kueleza tabia za watu ambao wamebarikiwa.

Mliobarikiwa

Neno "ninyi" ni wingi.

kusema kila aina ya mambo maovu dhidi yenu kwa uongo.

"watasema kila aina ubaya dhidi yenu" au "watasema mambo mabaya juu yenu ambayo si ya kweli"

kwa ajili yangu

"kwa sababu mwanifuata mimi" au "kwa sababu mwaniamini"

Furahini na kushangilia

"Furahini" na "kushangilia" humaanisha karibu kitu kile kile. Yesu alitaka wasikilizaji wake sio tu kufurahi bali hata kufanya zaidi kuliko kufurahi kama inawezekana.

Matthew 5:13

Sentensi unganishi

Yesu anaanza kufundisha juu ya jinsi wanafunzi wake walivyo kama chumvi na nuru.

Ninyi ni chumvi ya dunia

Inawezekana kumaanisha 1) kama vile chumvi inavyokifanya chakula kuwa kizuri, mwanafunzi wa Yesu yampasa kuwaathiri watu wa ulimwengu ili kwamba wawe wazuri au 2) kama vile chumvi iwezavyo kutumika kwa kutunza chakula, kadhalika wanafunzi wa Yesu wawalinde watu wasiharibike

Matthew 5:15

Pia watu hawawashi taa

"Watu hawawashi taa"

nakuiweka chini ya kikapu

"kuiweka taa chini ya kikapu." Hii ni kusema kuwa ni ujinga kutengeneza nwanga kwa lengo la kuufunika ili watu wasiuone mwanga wa taa.

Nuru yenu na ionekane mbele ya watu

Hii inamaanisha kuwa wanafunzi wa Yesu wanapaswa kuishi maisha ambayo yatawafnya wengine wajifunze kuhusu ukweli wa Mungu. "Maisha yenu yawe kama nuru iangazayo mbele ya watu.

Baba yenu aliye mbinguni

Ni vizuri zaidi ikitafsiriwa "Baba" kwa maana ya maneno sawa na yale yanayotumika kumaanisha baba wa katika mwili huu.

Matthew 5:17

Sentensi unganishi

Yesu anaanza kwa kufundisha jinsi alivyokuja kuitimiliza sheria ya agano la kale

manabii

Hii inamaanisha kile walichoandika manabii katika maandiko.

kweli nawaambieni

"Nawaambia ukweli" Kirai hiki kinaongeza nguvu juu ya kile Yesu atakachosema baadaye.

mpaka mbingu na dunia zote zipite

Hapa "mbingu" na "dunia" humaanisha ulimwengu wote. "Kama vile mbingu zidumuvyo"

hapana yodi moja wala nukta moja

"hapana hata ile herufi ndogo iliyoandikwa au sehemu ndogo ya herufi. Hii ni sitiari inayomaanisha kitu fulani katika maandiko kinachoweza kuonekana kuwa si cha muhimu. "wala sheria zinazoonekana kuwa si za muhimu

kila kitu kitakapokuwa kimetimizwa

Hiki kinaweza kuelezwa kwa kutumia mfumo tendaji. "Mambo yote yametokea" au "Mungu huyafanya mambo yote yatimie".

kila kitu

Kirai cha "kila kitu" kinamaanisha kila kitu kilicho kwenye sheria. "kila kitu kilicho kwenye sheria" au " kila kilichoandikwa kwenye sheria".

Matthew 5:19

yeyote avunjaye

"yeyote asiyetii" au "yeyote apuuziaye"

amri ndogo mojawapo ya amri hizi

"yeyote kati ya amri hizi, hata zile ndogo kabisa"

ataitwa

Hii inaweza kuelezeka kwa muunda tendaji. "Mungu atamwita mtu huyo" au "Mungu atawaita watu hao".

mdogo katika ufalme wa mbinguni

Kirai hiki kimetumika katika injili ya Mathayo tu. Kama inawezekana tumia "mbingu" katika tafsiri yako. "asiye na umuhimu kabisa kwenye ufalme wa Mungu" au "asiye na umuhimu katika utawala wa Mungu wetu wa mbingunij".

azishikaye na kuzifundisha

"anayetii amri zote hizi na kuwafundisha wengine kufanya hivyo hivyo"

mkubwa

"wa muhimu zaidi"

Kwa maana nawaambia

Hiki kinaongeza msisitizo kwa kile ambacho Yesu atasema baadaye.

nawa ... yenu ... hamta..

hivi ni viwakilishi vya wingi

haki yenu isipozidi haki ya waandishi n a mafarisayo, kwa vyovyote vile hamtaingia kataika ufalme wa mbinguni

Hii inaweza kuelezeka kwa muundo hai. "kwamba haki yenu lazima izidi... ili kuingia"

Matthew 5:21

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kufundisha jinsi alivyokuja kutimiliza sheria za agano la kale. Hapa anaanza kufundisha juu ya kuua na hasira

Maelezo kwa ujumla

Yesu anawaambia kikundi cha watu juu ya kile ambacho kinaweza kutokea kwao kama watu binafsi. Neno "mme" katika sentensi "mmesikia" na "nawaambia" ni maneno ya wingi. Ile amri ya "usiue"ni ya umoja, lakini unahitaji kuitafsiri katika wingi.

ilinenwa zamani

Hii inaweza kuelezeka kwa mfumo tendaji. "Mungu alisema na mababu zetu zamani za kale".

auaye yuko katika hatari ya hukumu

Hapa "hukumu" inamaanisha kuwa hakimu ndiye atakayemhukumu mtu kufa. "Hakimu atamhukumu yeyote amuuaye mtu mwingine"

kuua ... auaye

Neno hili linamaanisha kitendo cha mauji ya kudhamiria, na wala siyo kila aina ya mauji

Lakini nawambia

Kiwakilishi "na" kinatia msisitizo. Hii inamaanisha kuwa kile anachosema Yesu kina umuhimu sawa na amri itokayo kwa Mungu. Jaribu kutafsiri hili kataka mazingira yanayonesha msisitizo.

ndugu

Neno hili linamaanisha muumini mwenzetu

atakuwa katika hatari ya hukumu

Inaovyoonekana hapa Yesu hamaanishi hakimu wa kibinadamu bali Mungu anamhukumu mtu mwenye hasira kwa ndugu yake.

mtu usiyefaa ... mjinga

Hii ni mizaha kwa watu wasioweza kufifkiri kwa usahihi. "Mtu asiyefaa" ni sawa na "mtu asiye na akili," ambapo "mjinga" inaongezea wazo la kutokuwa mwaminifu kwa Mungu.

baraza

Yawezekana hili ni baraza dogo, siyo lile kuu.

Matthew 5:23

una

Yesu anawaambia kundi la watu juu ya kile kinachoweza kutokea kwao kibinafsi. matukio yote yanayohusiana na viwakilishi "una" na "yako" yametumika katika hali ya umoja, lakini lugha yako inaweza kukutaka utafsiri katika wingi

unatoa sadaka yako

"kutoa sadaka yako" au "kuleta sadaka yako"

katika madhabahu

Hii inamaanisha kuwa ni madhabahu ya Mungu iliyo hekaluni kule Yerusalemu, " madhabahuni pa Mungu hekaluni".

na unakumbuka kuwa

"na ukumbuke ukiwa umesimama madhabahuni"

ndugu yako ana jambo lolote dhidi yako

"mtu mwingine ana hasira na wewe kwa sababu ya kile ulichomfanyia"

kapatane kwanza na ndugu yako

Hili linaweza kuelezeka katika muundo tendaji. "jambo la kwanza ni kutafuta suluhu"

Matthew 5:25

Patana na... wako

Yesu anaongea na makutano juu ya kile kinachoweza kutokea katika hali ya mtu mmoja. Matukioyote ya viwakilishi vya "uki" na "wako" viko katika umoja, lakini lugha yako inaweza kukutaka uvitafsiri katika wingi.

mshitaki wako

Huyu ni mtu anayemtuhumu mtu kwa kufanya jambo fulani ambalo ni ovu. Anampeleka mtuhumiwa mahakamani ili kumshitaki kwa hakimu.

kukuacha mikononi mwa hakimu

Hapa neno "kukuacha mikononi mwa" inamaanisha kukukabidhi katika udhibiti wa mtu mwingine. "kumwachia hakimu ashughulike na wewe".

hakimu akuache mikononi mwa askari

Hapa neno "kukuacha mikononi mwa" inamaanisha kukukabidhi katika udhibiti wa mtu mwingine. "hakimu atamkabidhi kwa askari"

askari

ni mtu mwenye mamlaka ya kufanya maamuzi ya hakimu.

nawe utatupwa gerezani

Hili linaelezeka katika hali ya muundo tendaji. "na askari anaweza kukutupa gerezani"

amini nawambieni

"Nawaambieni ukweli." Hiki kirai kinaongeza msisitizo kwa kile ambacho Yesu alisema baadaye.

hutawekwa huru

"kutoka gerezani"

Matthew 5:27

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kufundisha juu ya jinsi alivyokuja kuitimiliza sheria ya Agano la Kale. Na hapa anaongelea uzinzi na kutamani mwanamke.

Maelezo kwa ujumla

Yesu anaongea na makutano juu ya kile kinachoweza kutokea katika maisha ya mtu binafsi. Neno "mme..." kutokana na "mmesikia" na "nawaambieni" yametumika katika wingi. Amri ya "Usizini" imetumika katika umoja "usi," lakini unaweza kuitafsiri katika wingi "msi".

imenenwa kuwa

Hii inaweza kuelezeka katika muundo tendaji. "kuwa Mungu alisema".

fanya (uzinzi)

Hili neno ni kitenzi kikuu cha kufanya jambo fulani

Lakini nawaambieni

Neno "nawa" ni msisitizo. Hii inamaanisha kuwa kile ambacho Yesu anasema kina umhimu sawa na kile kilicho kwenye amri kuu kotoka kwa Mungu. Tafsiri kirai hiki katika namna ambayo inaonesha msisitizo huo. Tazama ilivyotafsiriwa katika 5:21

yeyote amtazamaye mwanamke kwa kumtamani amekwisha kuzini naye moyoni mwake.

Sitiari hii inamaanisha kuwa mwanamume amtamaniye mwanamke anahatia sawa na mwanamume aliyefanya uzinzi halisi.

amtazamaye mwanamke kwa kumtamani

"na kumtamani mwanamke" au "na kutamani kulala naye"

moyoni mwake

Hapa "moyo" inamaanisha fikra za mtu. "akilini mwake" au "Katika fikra zake"

Matthew 5:29

Na kama ... lako

Yesu anaongea na makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye kwa mtu binafsi Matukio yote ya viwakilishi vya "ku" na "lako" viko katika umoja, lakini unaweza kuvitafsiri katika wingi.

kama jicho lako la kulia linakusababisha kujikwaa

Hapa "jicho" linamaanisha kile ambacho mtu hukiona. Na "kujikwaa". Ni sitiari ya "dhambi." "Kama kile ukionacho hukusababisha kujikwaa" au "kama unataka kufanya dhambi kwa sababu ya kile ukionacho"

jicho lako la kulia ... mkono wako wa kuume

Hii inamaanisha jicho au mkono ule wa muhimu zaidi, dhidi ya mkono au jicho la kushoto. Hapa unaweza kutafsri "kulia" kuwa "ndiyo nzuri zaidi" au "kulia pekee."

ling'oe

"litoe kwa nguvu" au "liharibu" kama jicho lako la kulia halijatajwa rasmi, unaweza kuitafsiri hii kama " kuharibu macho yako." kama macho yametajwa, unaweza kuyatafsiri kama "yaharibu"

ling'oe ... likate

Yesu analikuza zaidi jambo hili juu ya jinsi ambavyo mtu anapaswa kuiona jinsi dhambi ilivyo mbaya kulichukulia kwa umakini swala hili.

uutuplie mbali na wewe

"achana nao"

kiungo kimoja katika mwili wako kiharibike

"upoteze sehemu ya mwili wako"

kuliko mwili mzima kutupwa jehanamu

Hili linaweza kuelezeka katika muundo tendaji. "kuliko Mungu kuutupa mwili wako wote jehanamu"

kama mkono wako wa kuume unakusababisha

katika hii lugha ya umbo, mkono unasimama badala ya matendo la mwili wote

Matthew 5:31

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kufundisha juu ya jinsi alivyokuja kutimiliza sheria za Agano la kale. Hapa anaanza kwa kufundisha juu ya talaka

Imenenwa pia

Mungu ndiye "alisema." anatumia mfumo tendewa ili kuifanya kuwa laini kuwa si Mungu au neno la Mungu ambalo hakubaliani nalo. Badala yake anasema kuwa talaka inawezekana pale tu sababu ni ya kweli. talaka inaweza isikubalike hata kama mwanamume atatii kuandika hati ya talaka,

amfukuzaye mkewe

hii ni tafisida ya talaka

na ampe

"lazima ampatie"

lakini mimi nawaambia

Kiwakilishi "mimi" ni cha msisitizo. Hiki kinamaanisha kuwa anachosema Yesu kina umuhimu sawa na amri kuu kutoka kwa Mungu. Jaribu kutafsiri kirai hiki katika namna inayoonesha msisitizo. Tazama ilivyotafsiriwa katika 5:21.

Amfanya kuwa mzinzi

Ni mwanamume anayemtaliki mwanamke bila utaratibu humsababisha kufanya uzinzi" Katika tamadunii nyingi ni kawaida kwake kuolewa tena, lakini kama talaka hiyo haiko sahihi, basi hiyo ndoa ya pili ni batili.

baada ya kupewa talaka

Hii inaweza kuelezeka katika muundo tendaji. "yeye mwanamke baada ya kutalikiwa na mumewe" au "mwanamke aliyetalikiwa"

Matthew 5:33

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kufundisha juu ya jinsi alivyokuja kuitimiliza sheria ya Agano la kale. Na hapa anaanza kuongelea juu ya kuapa viapo

Maelezo kwa ujumla

Yesu anaongea na makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha ya mtu binafsi. Kiwakilishi "mme" kutokana na "mmesikia" na "nawaambia" viko kataka wingi. na kiwakilishi cha "msi" katika " msiape" na " ni" katika " pelekeni" navyo pia viko katika wingi

Tena, mme

"Pia, mme" au "huu ni mfano mwingine. wa kiwakilishi "mme."

mmesikis ilinenwa kwamba ... kwa uongo

Yesu anaweka bayana kuwa anakubaliana na Mungu na neno lake. Lakini, anawaambia wasikilizaji wake wasitimie vile amabvyo si vyao il ikuwashawishi watu kuamini maneno yao. "viongozi wenu wa dini wamewaambieni kuwa Mungu alisema ... viapo vya uongo.

Msiape kwa uongo, bali pelekeni viapo vyenu

Hi inaweza kumaanisha mambo yafuatayo 1)usiape kwa Mungu kuwa utafanya jambo fulani na usilifanye au 2) Usiape kwa jina la Bwana kuwa unajua kitu fulani kuwa ni kwe ili hali unajua kuwa si kweli.

Lakini nawaambia

Kiwaakilishi "na" ni cha msisitizo. Hii inamaanisha kuwa anachosema Yesu kina umuhimu sawa na kile kilicho kwenye amri kuu kutoka kwa Mungu. Kirai hiki kitafsriwe katika namna inayoonesha msisitizo. Tazama ilivyotafsiriwa katika 5:21

msiape hata kidogo ... ni mji wa mfalme mkuu

Hapa Yesu anamaanisha kuwa mtu asiape katika jambo lolote. inaonekana kuwa kuna mtu aliyekuwa akifundisha kwamba kuapa haina madhara kama mtu ataapa kwa kitu kingine na asikijali kiapo chake kama hakuapa kwa Mungu. ,kama vile kuapa kwa mbingu, dunia, au Yerusalemu. Yesu anasema hata kiapo cha hivyo ni kibaya kwa sababu vyote ni mali ya Mungu.

msiape hata kidogo

Kama lugha yako ina muundo wa wingi katika agizo inaweza kutumika hapa. "hamtaapa kwa kwa kiapo cha uongo" waruhusu watu watoe viapo lakini wazuieni viapo vya uongo. "msiape hata kidogo" hii inazuia viapo vya uongo.

kwa sababu ni enzi ya Mungu

Hapa neno "enzi" linamaanisha utawala wa Mungu kama mfalme. "linatokana chanzo hiki kwamba Mungu ni mtawala.

maana ni mahali pa kuweka kiti cha kukanyagia miguu yake

Kirai hiki kinamaanisha kuwa dunia ni mali ya Mungu. "ni kama mahali pa kuweka kiti cha kukanyagia miguu yake"

maana ni mji wa mfalme mkuu

"kwa maana ni mji unaomilikiwa na Mungu

Matthew 5:36

chako ... hu

Yesu anaongea na makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha yao binafsi. Matukio yote ya viwakilishi hivi viko katika umoja, lakini inakupass kuvitafsiri kama wingi.

kuapa

Hii inamaanisha kuapa. Tazama ilivyotafsiriwa katika 5:23

Bali maneno yenu yawe 'ndiyo, ndiyo,' au 'hapana. hapana'

kama unamaanisha 'ndiyo.' sema 'ndiyo,' na kama unamaanisha ;hapana,' sema 'hapana,'

Matthew 5:38

sentnsi unganishi

Yesu anaendelea kufundisha jinsi alivyokuja kuitimiliza sheria ya Agano la kale. Anaanza kwa kuongelea juu ya kisasi kwa maadui

Maelezo kwa ujumla

Yesu anaongea na makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha ya mtu kibinafsi. Kiwakilishi cha "mme" katika "mmesikia" na "mimi nawaambia" viko katika wingi. Kirai hiki "mtu akikupiga" kimesemwa katika umoja "akiku...," lakini unaweza kukitafsiri katika wingi "akiwa..."

mmesikia imenenwa kuwa

Yesu anakubaliana na Mungu na neno lake. Lakini hakubaliani na jinsi viongozi wa dini walivyolitumia neno la Mungu. "Viongozi wenu wa dini wamewambieni kuwa Mungu alisema." Tazama ilivyotafsiriwa katika 5:33

jicho kwa jicho na jino kwa jino

Sheria ya Musa ilimruhusu mtu kumwumiza kwa njia ileile kama alivyomwumiza, lakini hakumwumiza zaidiya kiasi kile

Lakini mimi nawaambia

Kiwakilishi cha "mimi" kinaongeza msisitizo. Hii inamaanisha kuwa alichosema Yesu kina umuhimu sawa na ule ulio kwenye amri kuu kuto kwa Mungu. Jaribu kutafsiri kirai hiki katika namna ambayo italeta msisitizo. Tazama ilivyotafsiriwa 5:21.

mtu mwovu

"ni mtu mwovu" au "mtu yeyote aliyewahi kukuumiza"

akikupiga shavu la kulia

Kumpiga mtu upande mmoja wa uso kilikuwa kitendo cha fedheha katika utamaduni wa Yesu. Kama ilivyo katika jicho na mkono, shavu la kulia ni la muhimu, kwa hiyo kukupiga shavu la kulia ilikuwa fedhaha kubwa mno.

akikupiga

"kuzabua," hii inammanisha kupiga kumpiga mtu kofi kwa ubapa wa mkono,

mgeuzie na jingine tena

"mwache akupige na shavu jingine pia"

Matthew 5:40

Maelezo kwa ujumla

Yesu anaongea na makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha ya watu binafsi. Viwakilishi vyote vya "wewe" na "yako" viko katika umoja kama vile amari za "mwachie," "nenda," "mpatie," na "usimwepuke," lakini waweza kuzitafsiri katika wingi.

kanzu ...joho

Hii "kanzu" ilivaliwa karibu na mwili, kama shati zito au sweta. "kanzu," hili lilikuwa la thamani zaidi kati ya haya mavazi mawili, ilivaliwa juu ya kanzu kwa ajili ya koongeza joto na pia lilitumika usiku kama blanketi.

mwachie na

"mpatie pia huyo mtu"

na yeyote

"na kama mtu," hii inamaanisha kuwa huyu ni askari wa Kirumi.

maili moja

Hizi na sawa na hatua elfu moja ambao ndiyo umbali ambao askari wa kirumi angeweza kumlazimisha kisheria mtu kubeba kitu kwa ajili yake. Kama maili moja haieleweki, basi inaweza kutafsiriwa kama "kilometa moja" au "umbali mrefu."

nenda naye

Hii inamhusu yule akulazimishaye kwenda.

nenda naye maili mbili

"uende ile maili anayokulazimisha kwenda, halafu nenda maili nyingine. kama "maili" haieleweki tumia kilometa mbili" au "mara mbili ya mwendo."

na usimwepuke yeyote

"usikatae kumpatia."hii inaweza kuelezeka kwa kutumia muundo halisi. "na umpatie"

Matthew 5:43

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kufundisha jinsi alivyokuja kuitimiliza sheria ya Agano la Kale. Hapa anaanza kufundisha juu ya kuwapenda maadui.

Maelezo kwa ujumla

Yesu anaongea na makutano juu ya kile kianachoweza kutokea kwao katika maisha yao kibinafsi. "Utampenda ... na kumchukia adui yako" maneno haya yametumika katika hali ya umoja, lakini unaweza kuyatafsiri katika wingi. Matukio mengine ya viwakilishi vya "u" na vile vya amri ya "umpende" na "omba viko katika wingi.

Mmesikia imenenwa

Yesu anakubaliana na Mungu na neno lake. Lakini hakubaliani na jinsi viongozi wa dini wanvyolitumia neno la Mungu. Hili linaweza kuelezeka katika muundo tendaji. "viongozi wenu wa dini wamewaambia kwamba Mungu alisema" Tazama ilivyotafsiriwa 5:33

jirani

Neno "jirani" hapa linamaanisha mtu ndani ya jamii ile ile au watu wa kundi moja ambao mtu hutamani na anapaswa kumtendea kwa upole. Haimaanishi mtu anayeishi karibu. Unaweza kutafsiri katika wingi.

Lakini nawaambia

Kiwakilishi "na.." kinatia msisitizo. Hii inaonesha kuwa kile anachokisema Yesu kina Uzito sawa na kile kilicho kwenye amri kuu ya Mungu.Jaribu kutafsiri kirai hiki kwa kutia msisitizo. Tazama ilivyotafsirwa katika 5:21

muwe watoto wa baba yenu

Ni vizuri kutafsiri "wana" katika lugha ambayo kwa asili hutumika kumaanisha baba wa watoto wa kimwili.

Baba

Hiki ni cheo cha muhimu cha Mungu

Matthew 5:46

Sentensi unganishi

Yesu anamaliza kufundisha juu ya jinsi alivyokuja kuitimiliza sheria ya Agano la kale. Kipengere hiki kinaanzia 5:17

Maelezo kwa ujumla

Yesu anaongea na makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha yao kibinafsi. Matukio yote ya viwakilishi vya "mki.." na "zenu" viko katika wingi. Maswali katika mistari hii ni yale usemaji ambao pengine si lazima kujibiwa

mkiwasalimia

Hili ni neno la jumla kwa ajili ya kuwatamanisha wasikilizaji.

Baba

Hiki ni cheo cha muhimu cha Mungu

Matthew 6

Mathayo 06 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Mathayo 6 inaendelea na mafundisho ya Yesu yaliyojulikana kama "Mahubiri ya Mlimani."

Labda mtafsiri atapenda kulitenga sala katika 6:9-11 kwa kutumia uingizaji. Kwa kuwa sura hii hubadilika haraka kutoka kwa mada moja hadi nyingine, inawezekana kutumia mstari wa nafasi kati ya mada tofauti ili kuwasaidia wasomaji kutambua mabadiliko katika mada kwa urahisi zaidi.

<< | >>

Matthew 6:1

Sentensi unganishi

Yesua anaendelea kufundisha wanafunzi wake katika mafundisho ya mlimani yanayoanzia 5:1.Katika sehemu hii, Yesu anahutubia juu ya "matendo ya haki" ya utoaji sadaka, maombi, na kufunga.

Maelezo kwa ujumla

Yesu anaongea na makutano juu kile kinachoweza kutokea kwao baadaye katika maisha yao binafsi. viwakilishi vyote vya "ni" na " yao" viko katika wingi.

mbele ya watu ili kujionyesha

Hii ilimaanisha kuwa wale wanaomuona mtu huyo watamheshimu. Hili linaweza kuelezeka katika mfumo tendaji. "mbele ya watu kwa kusudi la kutazamwa na watu ili wakupe heshima kwa kile ulichofanya."

Kweli nakwambia wewe

"Ninakuambia ukweli." Huu msemo unaongeza na kusisitiza kile ambacho Yesu atakisema baadaye.

Baba

Hii ni sifa muhimu ya Mungu

Usipige panda na kujisifu

Kirai hiki kina maanisha kitendo cha kukusudia kupata usikivu wa watu. "Usijipatie usikivu wa watu kwa lengo binafsi kama mtu anayepiga panda katikati ya watu.

kweli nawaambia

"Nawaambia ukweli." Kirai hiki kinaongeza msisitizo wa kile Yesu atakachokisema baadaye.

Matthew 6:3

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwafundisha wanafunzi wake juu ya sadaka

Maelezo kwa ujumla

Yesu anawaambia makutano juu ya kile kinachoweza kutokea kwao baadaye katika maisha binafsi. Viwakilishi vya "wewe" na " ""wako" viko katika wingi.

mkono wako wa kushoto usijue kinachofanywa na mkono wa kulia

Huu ni msemo unaonyesha usiri. Kama vile mikono inavyofanya kazi pamoja na inasemekana "kujua" kila kitu kinachofanywa kwa wakati wote, hivyo hata watu wako wa karibu wasijue unapotoa msaada kwa maskini

sadaka yako itoe kwa siri

Hii inaweza kuelezeka kwa mfumo tendaji "utawapa maskini pasipo watu wengine kujua."

Matthew 6:5

Sentensi unganishi

Yesu anaanza kufundisha juu ya maombi

Maelezo kwa ujumla

Yesu anaongea na makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha binafsi.. Viwakilisha vya "una" na "yao" katika mstari wa 5 na 6 viko katika wingi: katika mstari wa 6 viko katika umoja lakini waweza kuvitafsiri katika wingi.

ili kwamba watu wawatazame

Inamaanisha kwamba wale wanaowatazama watawapa heshima. Hii inaweza kuelezeka kwa mfumo tendaji"ili kwamba watu wawatazame wao na kuwapa heshima."

kweli ninawaambia

ukweli ninakuambia." Huu msemo jnaongeza na kusisitiza kile ambacho Yesu atakisema baadaye'

ingia chumbani. Funga mlango

"nenda sehemu ya usiri" au "nenda sehemu ambayo utakuwa peke yako"

Baba aliye sirini

Tafsiri inayowezekana ni 1) hakuna anayeweza kumwona Mungu au 2) Mungu yuko sehemu ya siri pamoja na mtu anayeomba.

Baba

Hii ni sifa muhimu ya Mungu

Baba yako aonaye sirini

Baba yako ataona kile ufanyacho sirini"

kurudia yasiyo na maana

"kurudia maneno yasiyo na maana"

watasikiwa

Hii inaweza kuelezeka kwa mfumo tendaji. "miungu yao ya uongo itawasikiliza"

maneno mengi

sara ndefu" au "maneno mengi"

Matthew 6:8

Maelezo kwa ujumla

Yesu anaongea na makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha binfsi. anawaambia kama kundi kwa kutumia wingi kama vile "ombeni hivi." viwakilishi vyote vya "lako" baada ya "baba yetu uliye mbinguni" viko katika umoja.

Baba

Hii ni sifa muhimu ya Mungu

ulitakase jina lako

Hapa "jina" linamaanisha Mungu mwenyewe. "linamfanya kila mmoja kujua yeye ni mtakatifu."

ufalme wako uje

Hapa "ufalme" inamaanisha utawala wa Mungu kama mfalme. AT: "Waweza kutawala juu ya yote na kila kitu kikamilifu"

mapenzi yako yafanyike hapa duniani kama huko mbinguni

Hii inaweza kuelezeka kwa mfumo hai. AT: "Kila mmoja duniani atii mapenzi yako kama wanavyofanya kila mmoja huko mbinguni."

Matthew 6:11

Maelezo kwa ujumla

Mionekano ya viwakilishi vya "nasi," "utu," "wetu" unaonesha makutano ambao Yesu alikuwa akiwahutubia.

mkate wa kila siku

Hapa "mkate" inamaanisha chakula kwa ujumla,

deni

Deni ni kile ambacho mtu anamdai mwingine. Huu ni msemo wa dhambi.

wadeni

Mdai ni mtu ambaye anadai deni kwa mwingine. Huu ni msemo kwa wenye dhambi.

usitulete katika majaribu

Neno "majaribu" jina la kitenzi, inaweza kuelezwa kama kitenzi. "usituletee kitu chochote cha kutujaribu" au "usituletee kitu cha kutufanya tushawishike na dhambi"

Matthew 6:14

Maelezo kwa ujumla

viwakilishi vyote vya "mta" na "yako" ni vya wingi. hata hivyo, Yesu anawaambia kile kitakachotokea baadaye katika maisha binafsi kama kila mmoja hatasamehe wengine

maovu

"makosa" au "dhambi"

Baba

Hii ni sifa muhimu ya Mungu

Matthew 6:16

Sentensi unganishi

Yesu anaanza kufundisha juu ya kufunga

Maelezo kwa ujumla

Yesu anawaambia makutano juu ya kile kinachoweza kutokea katika maisha yao binafsi. Viwakilishi vyote vya "una" na "zao" katika mstari wa 17 na 18 viko katika umoja, lakini vinaweza kutafsiriwa katika wingi ili vioane na kile cha "wa" katika mstari wa 16.

Aidha

"Zaidi ya"

wanakunja sura zao

Wanafiki hawakuosha nyuso zao au kuchana nywele zao. Walifanya hivyo makusudi kuvuta hisia zao ili kwamba watu wawatazame wao na kuwapa heshima kwa sababu ya kufunga.

kweli ninakuambia

"Ukweli ninakuambia." Huu msemo unaongeza na kusisitiza kile ambacho Yesu atakiongea baadaye.

tengeneza kichwa chako

"paka mafuta kwenye nywele zako" au "tengeneza nywele zako" Kutunza kichwa hapa ni hali ya kawaida ya kutunza nywele. Halina uhusiano na "Kristo" ikimaanisha "mpakwa mafuta" Yesu alikuwa anamaanisha kwamba watu wanapaswa kuonekana kawaida haijalishi wamefunga au hawakufunga.

Baba aliye sirini ... yeye anayeona sirini

Tazama unavyotafsiri hii kwenye 6:5

Baba

Hii ni sifa muhimu ya Mungu

aonaye sirini

"Aonaye kile unachokifanya unapokuwa pekee yako" Tazama ilivyotafsriwa katka 6:5

Matthew 6:19

Sentensi unganishi

Yesu anaanza kufundisha juu ya fedha na mali

Maelezo kwa ujumla

Yesu anawaambia makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha yao binafsi. viwakilishi vya "usi" na "yako" viko katika wingi isipokuwa vile vya mstari wa 21, amabvyo viko katika umoja.

akiba

"utajiri"

ambapo nondo na kutu wanakula

"ambapo nondo na kutu wanashambulia akiba"

nondo

mdudu mdogo, anayeruka na kuharibu nguo

kutu

ni vitu vya rangi ya kahawia vinavyopatikana kwenye chuma

weka akiba yako mbinguni

Huu ni msemo ambao unamaanisha kwamba fanya mambo mazuri hapa duniani ili Mungu akubariki mbinguni.

na moyo wako utakapokuwepo pia.

Hapa "moyo" maana yake ni mawazo ya mtu na mapenzi yake.

Matthew 6:22

Maelezo kwa ujumla

Yesu anawaambia makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha yao binafasi. viwakilishi vya "yako" vimo katika umoja lakini waweza kuvitafsiri katika wingi.

Jicho ni taa ya mwili... hilo giza ni kubwa kiasi gani

Hii inalinganisha macho mazima ambayo yanamwezesha mtu kuona macho mabovu ambayo yanasababisha mtu kuwa kipofu. Huu ni msemo unaomaanisha uzima wa kiroho. Mara nyingi, wayahudi walitumia msemo "macho mabaya" wakimaanisha uovu. Maana yake ni hii ikiwa mtu amejitoa kwa Mungu na kuona vitu vinafanyika kwa njia hiyo wanafanya vizuri. Endapo mtu ana tamaa ya utajiri wa vitu vingine hivyo anafanya uovu.

jicho

Unaweza kutafsiri kwa wingi, "macho"

ikiwa jicho lako ni baya

Hii aimanishi maajabu. Wayahudi mara zote walitumia msemo huu kwa mtu ambaye ni mwovu.

kwa kuwa atamchukia mmoja na kumpenda mwingine, au la sivyo atajitoa kwa mmoja na kumwachaniza mwingine

Yote kwa pamoja kimsingi yana maana moja. Yanasisitiza kwamba mtu hawezi kupenda na kujitoa kwa Mungu na fedha kwa wakati mmoja.

Huwezi kumtumikia Mungu na mali

"Huwezi kumpenda Mungu na fedha kwa wakati mmoja"

Matthew 6:25

Maelezo kwauumla

Hapa viwakilishi vya "ku" na "yako" vyote viko katika wingi

Ninakuambia wewe

Hii inaongeza msisitizo kwa kile atakachosema Yesu baadaye

kwako

Yesu anaongea kwa kikundi cha watu kuhusu kitakachotokea kwao kwa mtu binafsi. Anapotumia "kwako" na "wako" yote ni wingi.

maisha si zaidi ya chakula na mwili zaidi ya mavazi?

Yesu anatumia swali kufundisha watu. "uhakika maisha ni zaidi ya kile unachokula, na mwili wako ni zaidi ya kile unachovaa."

ghala

sehemu ya kutunza mazao

Baba

Hii ni sifa muhimu ya Mungu

Je ninyi hamna thamani kuliko wao?

Yesu anatumia swali kufundisha watu. "uhakika ninyi mna thamani zaidi ya ndege."

Matthew 6:27

Maelezo kwa ujumla

Yesu ansema na makutano juu ya kile kinachoweza kutokea kwao katika maisha binafsi.viwakilishi vya "mwenu" na "yake" vimo katika wingi.

Na nani mmoja miongoni mwenu kwa kuwa na wasiwasi anaweza kuongeza siku za kuishi?

Yesu anatumia swali kufundisha watu. Anamaanisha hakuna atakayeishi maisha marefu kwa kuwa na hofu.

inchi moja

"inchi" ni pungufu ya mita. Hapa ni msemo wa kuongeza kiasi cha miaka mingapi ya kuishi mtu.

Na kwa nini mna kuwa na hofu kuhusu mavazi?

Yesu anatumia swali kufundisha watu. AT:"Usiwe na hofu kuhusu nini utavaa."

Fikiria kuhusu

'Zingatia"

maua

aina ya maua ya porini

Ninakuambia wewe

Hii inaongeza msisitizo wa kile ambacho Yesu ataongea baadae

hakuwahi kuvikwa kwa namna hii

Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai. AT:"hakuvaa nguo nzuri kama haya maua."

Matthew 6:30

Maelezo kwa ujumla

Yesu anawaambia makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha yao kibinafsi. viwakilishi vya "ninyi" na "wenye" vimo katika wingi.

anayavalisha majani

Huu ni msemo ukiwa na maana Mungu anayapendezesha maua

majani

Ikiwa lugha yako ina neno linalohisi "majani" na neno ulilotumia kwa "maua" kwa mstari uliopita, unaweza kutumia hapa.

yanatupwa na kuteketea

Wayahudi tena walitumia majani kwa moto na kupikia vyakula vyao. Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai. "mtu mmoja alitupa katika moto" au "mtu mmoja alichoma"

ni kwa kiwango gani atawavalisha ninyi ....imani?

Yesu anatumia swali kufundisha watu.AT: yeye hakika atawavisha ninyi...imani."

ninyi wenye imani ndogo

"ninyi ambao mna imani ndogo." Yesu anawatuhumu watu kwa sababu walikuwa na imani ndogo na Mungu.

Hivyo basi

"Kwa sababu ya hayo yote"

Matthew 6:32

Kwa kuwa mataifa wanafuta mambo haya

"kwa mataifa wanajali san juu ya kile watachokula, kunywa na kuvaa"

Baba yenu wa mbinguni anajua mnahitaji hayo

Yesu anamaanisha kwamba Mungu atahakikisha mahitaji ya muhimu mnapata

Baba

Hii ni sifa muhimu ya Mungu

tafuta kwanza ufalme na haki

Hapa "ufalme" inamaanisha utawala wa Mungu kama mfalme. "umaanishe mwenyewe katika kumtumikia Mungu, ambaye ni mfalme wako, na ufanye yaliyo haki."

hayo mengine yote atakupatia wewe

Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai.AT: "Mungu atakupatia hayo yote wewe."

Hivyo basi

"Kwa sababu ya hayo yote"

kesho itajua yenyewe

Yesu anafafanua "kesho" kama mtu ambaye anaweza kuhofu. Yesu anamaanisha kwamba mtu anaweza kuhofu endapo siku inayofuata imefika.

kila siku ina tatizo la kujitosheleza yenyewe

"kila siku huwa ina mabaya yake yakujitosheleza" au "Kila siku ina matatizo yake ya kutosha"

Matthew 7

Mathayo 07 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Kwa kuwa sura hii hubadilika haraka kutoka kwa mada moja hadi nyingine, inawezekana kutumia mstari wa nafasi kati ya mada ili kutofautisha kati yao kwa urahisi zaidi.

Dhana maalum katika sura hii

Mathayo 5-7

Mathayo 5-7 kwa pamoja huunda mahubiri au mafundisho ya Yesu. Mgawanyiko wa sura husababisha kuchanganyikiwa hapa.

"Utawajua kwa matunda yao"

Matunda ni taswira ya kawaida katika maandiko. Inatumika kuelezea matokeo ya tabia nzuri au mbaya. Katika sura hii, matunda mazuri ni matokeo ya kuishi kama Mungu anavyoamuru. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#fruit)

<< | >>

Matthew 7:1

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwafundisha wanafunzi wake katika mahubiri ya mlimani, yanayoanzia 5:1

Maelezo kwa ujumla

Yesu anawaambia makutano juu ya kile kinachoweza kutokea kwao baadaye katika maisha binafsi. viwakilishi vya "nawe" na amri viko katika wingi.

Usihukumu

Inamaanisha hapa kwamba "hukumu" ina maana ya msingi kuwa "kushutumu vibaya" au "kutangaza kosa"AT:"Usishutumu watu vibaya."

nawe usije ukahukumiwa

Hii inaweza kutafsiriwa kwa mfumo hai.AT:"Mungu hawezi kukushutumu wewe vibaya."

Kwa

Uwe na uhakika msomaji anaelewa maelezo ya mstari wa 7:2 uwe na msingi alichokisema Yesu katika wa 7:1

kwa hukumu utakayohukumu, nawe utahukumiwa

Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai.AT: "Mungu atakushutumu wewe hivyo hivyo kama

kipimo

Tafsiri inayowezekana ni 1) hii ni kipimo cha hukumu unayopewa au 2) hiki ni kiwango kinachotumika kwa kuhukumu.

utapimiwa hicho hicho

Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai. "Mungu atatumia kipimo hicho kwako."

Matthew 7:3

Maelezo kwa ujumla

Yesu anawaambia makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha yao binafasi. viwakilishi vya "u" na "yako" vimo katika umoja lakini vinaweza kutafsirika katika wingi.

kwa nini unatazama....Unawezaje kusema

Yesu anatumia maswali yote kufundisha na kutoa changamoto kwa watu. Yeye anataka wao wajiangalie dhambi zao kabla ya kuangalia dhambi za mtu mwingine.

kipande cha mti

ni msemo

kaka

Hii inamaanisha mkristo mwenzako, siyo kaka halisi au jirani

kipande cha mti

Sehemu ya kipande kikubwa cha mti ambacho mtu amekikata chini. Ni kipande cha ubao kwa mbali kikubwa kiualisia kimeingia kwenye jicho la mtu. Huu ni msemo muhimu kwa mtu mwenye makosa

Matthew 7:6

Maelezo kwa ujumla

Yesu anawaambia makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha yao binafsi. viwakilishi vya "u" na "yao" viko katika wingi.

mbwa....nguruwe

Wayahudi waliwachukulia wanyama hawa kuwa wachafu, na Mungu aliwaambia wayahudi wasiwale. Huu ni msemo kwa watu waovu ambao hawathamini vitu vitakatifu. Itakuwa vizuri kutafsiri maneno haya kiualisia.

lulu

Hiki ni sawa na mviringo,jiwe la thamani au glasi. Ni misemo ya elimu ya Mungu au vitu vyenye ubora kiujumla.

wanaweza kuviharibu

"nguruwe wataviharibu"

na tena watageuka na kurarua

"na mbwa watageuka na kurarua"

Matthew 7:7

Maelezo kwa ujumla

Yesu anawaambia makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha yao binafsi. viwakilishi vya "wewe" na "wake" wake katika wingi.

Omba...Tafuta...Bisha

Hii ni misemo ya maombi kwa Mungu. Mfumo wa kitenzi inaonyesha kwamba tuendelee kuomba mpaka yeye ajibu. Ikiwa lugha yako ina mfumo wa kufanya kitu na kurudia rudia tena, unaweza kutumia hapa.

Omba

Hii ina maana ya kuhitaji kitu kutoka kwa Mungu

Nawe utapewa

Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai.AT:"Mungu atakupa kile unachotaka."

Tafuta

"Tafuta kutoka kwa Mungu kile unachotaka"

Gonga

Kugonga mlango ilikuwa njjia ya upole ya kumwomba mtu aliye ndani ya nyumba au chumba afungue mlango.Ikiwa kugonga mlango si kwa upole kwenye utamaduni wenu, tumia neno ambalo linaelezea kwa upole mtu anapotaka kufunguliwa mlango.

nawe utafunguliwa

Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo tendaji. Mungu atakufungulia kwa ajili yako"

au kuna mtu miongoni mwenu ambaye....jiwe?

Yesu anatumia swali kufundisha watu. "Hakuna mtu miongoni mwenu ... jiwe,"

kipande cha mkate

Hii inamaanisha chakula kwa ujumla. "chakula"

jiwe...samaki...nyoka

Haya majina yatafsiriwe kiualisia.

au ikiwa atamwomba samaki, na yeye atampa nyoka?

Yesu anauliza swali jingine kufundisha watu. Inaeleweka kwamba yesu alikuwa anarejea mtu na kijana wake. "Na hakuna mtu miongoni mwenu, ikiwa kijana amemwomba samaki, atampatia nyoka."

Matthew 7:11

Maelezo kwa ujumla

Yesu anawaambia makutano juu ya kile kinachoweza kutokea baadaye katika maisha yao binafsi. Viwakilishi vya "ninyi" na :wenu" ni vya wingi.

ni kwa kiasi gani zaidi Baba aliye mbinguni atawapa...... yeye?

Yesu anatumia swali kujibu watu. "ndipo Baba yenu aliye mbinguni hakika atampa....yeye."

Baba

Hii ni sifa muhimu ya Mungu.

unataka kufanyiwa kitu chochote na watu

kwa njia yeyote lolote unalotaka ufanyiwe na wengine"

kwa kuwa hiyo ni sheria na unabii

Hapa "sheria" na "unabii" kinarejea kile ambacho Musa na manabii walikiandika. kwa kuwa hiki ndicho kile Musa na manabii walifundisha kwenye maandiko."

Matthew 7:13

Maelezo kwa ujumla

unapotafsri, tumia neno sahihi la "pana" na la "pana sana" kama yanavyotofautiana na "embamba" kama inavyowezekana ili kukazia tofauti ya hizo jozi za malango na njia.

Ingia kwa kupitia njia nyembamba...wachache wanaoweza kuiona

Hiki ni kivuli cha mtu anayetembea njiani na kuingia kwenye ufalme kwa kupita lango. Ufalme mmoja ni rahisi kuingia na mwingine si rahisi kuingia. Huu ni msemo unaomaanisha kwamba mtu anapaswa kukubali njia ngumu ya maisha ya kumtii Mungu na kupata uzima wa milele. Ikiwa watachagua njia nyepesi ya maisha ya kutomtii Mungu, wataingia kuzimu.

Ingia kwaa kupitia njia nyembamba

Unatakiwa kuendelea hadi mwisho wa mstari wa 14: "Hivyo basi, ingia kwa kupitia njia nyembamba."

lango.....njia

Tafsiri inayowezekana ni 1) hii inarejea langoi la kuingia katika ufalme na njia inayoongoza kwenye lango. Ikiwa hivyo, unaweza kubadilisha mpangalio kinyume kama walivyofanya UDB au 2) "lango" na "njia" vyote vinarejea lango la ufalme. ikiwa hivyo, una haja ya kubadili mpangilio.

katika uharibifu.... katika uzima

Haya majina ya sifa yanaweza kutafsiriwa kwa vitendo. "katika eneo ambalo utakufa.... katika eneo ambalo utaishi."

Matthew 7:15

Jihadharini na

"jilindeni na"

wanakuja wamevaa ngozi ya kondoo,lakini kweli ni mbwa wakali

Huu msemo una maana manabii wa uongo watajifanya wazuri na kutaka kuwasaidia, lakini kwa ualisia ni waovu na watawadhuru.

Kwa matunda yao utawatambua

Huu msemo unarejea matendo ya mtu. "Kama vile unavyofahamu mti kwa tunda linalotokea, utamtabua nabii wa uongo kwa matendo yao."

Je watu wanaweza kuvuna ....miiba?

Yesu anatumia swali kujibu watu. Watu wangetambua kwamba jibu siyo. "watu hawezi kuvuna...miba."

kila mti mzuri huzaa matunda mazuri

Yesu anaendelea kutumia msemo wa tunda akimaanisha nabii mzuri ambaye anafanya kazi nzuri au maneno mazuri.

mti mbaya huzaa matunda mabaya

Yesu anaendelea kutumia mfano wa matunda kwa kurejea kwa nabii mbaya ambaye anafanya kazi ya uovu.

Matthew 7:18

Kila mti ambao hauzai matunda mazuri utakatwa na kutupwa katika moto.

Yesu anaendelea kutumia mti wa matunda kama msemo akimaanisha manbii wa uongo. Hapa, yeye anaongelea kile kitakachotokea kwa mti mbaya. Ikimaanisha kwamba kitu hicho kitafanyika kwa manabii wa uongo.

itakatwa chini na kutupwa katika moto

Hii inaweza kuelezeka kwa mfumo hai. "mtu ataukata chini na kuuchoma."

kwa matunda yao mtawatambua

Neno "yao" inaweza kurejea labda manabii au miti. Huu msemo unamaanisha kwamba matunda ya mti na matendo ya manabii yote yanafunua kuwa yaweza kuwa mabaya au mazuri. Kama ikiwezekana, unaweza kutafsiri ikimaanisha maana moja kati ya hayo'

Matthew 7:21

wataingia katika ufalme wa mbinguni

Hapa "ufalme" inamaanisha utawala wa Mungu kama mfalme. Msemo "ufalme wa mbinguni" umetumika pekee katika kitabu cha mathayo. Ikiwa inawezekana, andika "mbingu" katika tafsiri yako. "wataishi pamoja na Mungu mbinguni pindi atakapojifunua kuwa mfalme."

wale wanaotenda mapenzi ya Baba

"wale wanaotenda kile ambcho Baba yangu anataka"

Baba

Hii ni sifa muhimu ya Mungu

siku hiyo

Yesu alisema "siku hiyo" akijua wasikilizaji walielewa alichomaanisha siku ya hukumu. Unaweza kuhusisha "siku ya hukumu" endapo tu wasikulizaji wako hawatakuelewa vinginevyo.

hatukutoa unabii....kutoa mapepo...tulifanya miujiza mingi?

Watu walitumia maswali kusisitiza kwamba walifanya mambo hayo. "tulitabiri..tulitoa pepo...tulifanya miujiza mingi."

sisi

Hii "sisi" haimuhusishi Yesu.

kwa jina lako

Hapa "jina" maana yake katika nguvu na mamlaka ya Yesu

matendo ya ajabu

"miujiza"

sikuwatambua ninyi

Hii ina maana mtu huyu si wa Yesu."Wewe si mfuasi wangu" au "Sina kitu cha kufanya pamoja nawe"

Matthew 7:24

Hivyo basi

"Kwa sababu hiyo"

maneno yangu

Hapa "maneno" yanarejea kile ambacho Yesu alisema

kama mtu mwenye hekima aliyejenga nyumba juu ya mwamba

Yesu analinganisha wale wanaotii neno lake na mtu aliyejenga nyumba ambayo haitazulika na kitu.

mwamba

Huu ni mwamba mbaya chini ya mchanga ulio juu na udongo, sio jiwe kubwa au mpaka juu ya ardhi.

ilikuwa imejengwa

Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo tendaji. "yeye alijenga"

Matthew 7:26

Sentensi unganishi

Huu ndio mwisho wa mahubiri ya Yesu ya mlimani yanayoanzaia 5:1

atafananishwa na mtu mpumbavu aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga

Yesu aliendelea kutumia mlinganyo kutoka mstari uliopita. Yeye analinganisha wale ambao hawatii neno lake na mpumbavu aliyejenga nyumba. Mpumbavu pekee aweza kujenga nyumba juu ya mchanga ambapo mvua,mafuriko na upepo vinaweza kuhamisha mchanga.

kuanguka

Tumia neno la ujumla kwa lugha yako ambalo linaelezea kilichotokea wakati nyumba inaanguka chini.

na anguko lake likakamilika

Mvua,mafuriko na upepo hakika yaliangamiza nyumba.

Matthew 7:28

Maelezo kwa ujumla

Mistari hii inafafanua jinsi watu katika makutano walivyoyapokea mafundisho ya Yesu ya mlimani.

ilifika kipindi ambacho

Huu usemi unaonyesha hitimisho la hotuba ya mlimani.

walishangazwa kwa mafundisho yake

iko wazi katika 7:29 kwamba walishangazwa si kwa sababu ya alichofundisha Yesu bali pia jinsi alivyofundisha . "walishangazwa kwa jinsi alivyoweza kufundisha."

Matthew 8

Mathayo 08 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Sura hii inaanza sehemu mpya.

Dhana maalum katika sura hii

Miujiza

Miujiza ya Yesu katika sura hii inaonyesha kwamba ana mamlaka juu ya mambo yanayopita udhibiti wa binadamu. Inaonyesha pia kwamba kumwabudu Yesu ni jibu sahihi kwa matendo yake. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#authority)

<< | >>

Matthew 8:1

Maelezo kwa ujumla

Huu ni mwanzo wa sehemu mpaya ya simulizi ambalo limebeba simulizi nyingi za uponya wa watu. Wazo hili linaendelea hadi hadi 9:35.

Wakati Yesu alipokuja kushuka chini kutoka mlimani, umati mkubwa ulimfuata.

"Baada ya Yesu kuja kushuka chini kutoka mlimani, umati mkubwa ulimfuata," Umati yawezekana ulijumuisha watu waliokuwa nae juu mlimani na watu ambao hawakuwahi kuwa nae.

Tazama

Neno "tazama" inatupa dokezo sisi la mtu mwingine katika hadithi. Lugha inaweza kuwa namna ya kufanya hivyo.

mkoma

"mtu ambaye ana ukoma" au "mtu ambaye ana ugonjwa wa ngozi"

kusujudu mbele yake

Hii ni ishara ya unyenyekevu heshima mbele ya Yesu.

Ikiwa unataka

"ikiwa unataka kufanya" au "ikiwa unahitaji" mwenye ukoma alijua yesu ana nguvu za kumponya, lakini hakujua endapo Yesu alitaka kumgusa yeye.

wewe unaweza kunisafisha

Hapa "kusafisha" maana yake kuponywa na ili kuweza kuishi kwenye jamii tena."

mara moja

"sasa hivi"

naye akasafishwa ukoma wake

Matokeo ya Yesu kusema"Uwe mzima" ilikuwa kwamba mtu huyo akaponywa.Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai.AT:"yeye alikuwa mzima" au "ukoma ulimwacha" au "ukoma ulikoma"

Matthew 8:4

yeye

Hii alikuwa anarejea mtu ambaye alimponya

usimwambie mtu yeyote

"usiseme kitu chochote kwa mtu yeyote" au "usimwambie mtu yeyote nimekuponya wewe"

ukajionyeshe kwa makuhani

Sheria ya wayahudi ililazimu kwamba mtu akaonyeshe ngozi aliyoponywa kwa kuhani, ambaye tena angemruhusu yeye au yule kuwa pamoja na watu wengine.

utoe zawadi ambayo Musa aliwaagiza,kwa ajili ya ushuhuda kwao.

Sheria ya Musa ililazimu kwamba yeyote aliyeponywa ukoma atoe sadaka ya shukrani kwa kuhani. Endapo kuhani atakubali zawadi, watu watajua kwamba mtu huyo ameponywa.

kwao

Hii kwa uhakika inaweza kurejea kwa 1) makuhani au 2) wapingaji wa Yesu. Ikiwezekana, tumia kiwakilishi ambacho kitaonyesha kati ya makundi hayo.

Matthew 8:5

Sentensi unganishi

Hapa simulizi hili linabadili mandhari ya muda na eneo na simulizi inakuwa ni ya habari za Yesu akimponya mtu mwingine

akaja kwake na kumwambia yeye

Hapa "yeye" anarejea kwa Yesu.

amepooza

"Asiyeweza kutembea kwa sababu ya ugonjwa"

Yesu akamwambia yeye

"Yesu akamwambia jemedari"

nitakuja na kumponya yeye

"nitakuja nyumbani kwako na kumfanya mtumishi wako apone"

Matthew 8:8

kuingia ndani ya dari langu

Msemo "kuingia ndani ya dari" maana yake "nyumba yangu"

sema neno

Hapa "neno" maana yake sema amri.AT: "toa amri"

ataponywa

Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai.AT: "atakuja kuwa mzima"

walio chini ya mamlaka

Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai.AT:"ambaye yuko chini ya mamlaka ya mwingine"

chini ya mamlaka...... chini yangu

Kuwa "chini" mtu inamaanisha kutokuwa na umuhimu sana na kutii agizo la mtu mwenye umuhimu zaidi.

mwanajeshi

"mtalaamu wa kupigana"

kweli ninawaambia

"Ninawaambia ukweli." Huu usemi unaongeza na kusisitiza kile ambacho yesu atazungumza baadae.

sijapata kuona mtu mwenye imani kama huyu Israel

Wasikilizaji wa Yesu wangefikiri kwamba wayahudi katika Israeli, ambao wanadai kuwa ni watoto wa Mungu, watakuwa na imani kuliko yeyote. Yesu anasema hawako sahihi na kwamba imani ya jemedari ilikuwa kubwa.

Matthew 8:11

wewe

Hapa "wewe" ni wingi na ina maanisha "wale ambao walikuwa wakimfuata yeye"

kutoka mashariki na magharibi

Unapotumia kinyume "mashariki" na "magharibi" ni njia ya kusema "kila mahali," "kutoka kila mahali" au "kutoka mbali kila upande"

wataketi katika meza

watu katika utamaduni walikaa chini pembeni ya meza wakiwa wanakula. Huu msemo unaonyesha kwamba wale walio mezani ni familia na marafiki wa karibu. "ishi kama familia na rafiki."

katika ufalme wa mbinguni

Hapa "ufalme" ina maanisha utawala wa Mungu kama mfalme. Msemo "ufalme wa mbinguni" umetumika katika kitabu cha Mathayo. Ikiwezekana, andika "mbinguni" katika tafsiri yako. "wakati Mungu wetu mbinguni anaonyesha kwamba yeye ni mfalme."

watoto katika ufalme watatupwa

Hii inaweza kuelezwa katika mfumo hai. "Mungu atawatupa watoto katika ufalme."

watoto katika ufalme

Usemi "watoto wa"ina maanisha wale ambao wanamikiwa na kitu fulani, kwa namna hiyo ufame wa Mungu. Kuna kejeli pia hapa kwa sababu "watoto" watatupwa nje wakati wageni watakaribishwa. "wale ambao waliruhusu Mungu awatawale wao."

nje gizani

Haya maelezo yanamaanisha hatua ya mwisho ya milele kwa wale waliomkataa Mungu. "sehemu ya giza mbali kwa Mungu" au "kuzimu"

itendeke hivyo kwako

Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai. "hivyo nitafanya kwa ajili yako wewe"

mtumishi aliponywa

Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai. "Yesu alimponya mtumishi"

kwa wakati huo

kwa muda ule Yesu alisema yeye atamponya mtumishi."

Matthew 8:14

Sentensi ungsnishi

Hapa simulizi inabadili mandhari ya muda na eneo. simulizi inakuwa ni ya Yesu akimponya mtu mwingine

Yesu alipofika

Hawa wanafunzi yawezekana walikuwa na Yesu, lakini mtazamo wa hadithi Yesu alisema nini na kufanya nini, hivyo watambulishe wanafunzi pekee ikiwa inalazimika kuepusha maana ya uongo.

Mama mkwe wa Petro

Mkwe - "mama wa mke wa Petro"

homa ikamwacha

Ikiwa lugha yako itaelewa msemo kuwa homa inaweza kufikiri na kutenda yenyewe, hii inaweza kutafsiriwa kama "yeye akawa mzima" au "Yesu akamponya yeye:

akaamka

"akaamka toka kitandani"

Matthew 8:16

Sentensi unganishi

Mandhari yanahamia katika muda wa jioni ambapo Simulizi inakuwa ya Yesu kuponya watu zaidi na kufukuza mapepo..

Maelezo ya jumla

Katika mstari wa 17, mwadishi anamnukuu nabii Isaya il ikuonesha kuwa huduma ya Yesu ilikuwa kutimiza unabii.

Na ilipofika jioni

Hii inajulisha kwamba hii ni baada ya Sabato, kwa sababu wayahudi walikuwa hawafanyi kazi au kusafiri siku ya Sabato. Walisubiri muda wa jioni kuleta watu kwa Yesu. Hauhitaji kutaja Sabato isipokuwa unataka kuepuka tafsiri ya uongo

wengi waliotawaliwa na mapepo

Hii inaweza kutafsiriwa kwa mfumo hai.AT:"wengi ambao mapepo yaliwatawala" (UDB) au "wengi ambao walipagawa na mapepo"

Naye akawafukuza roho kwa neno

Hapa "neno" inamaanisha amri. Yeye aliwaamuru pepo kuondoka."

yalitimizwa unabii wa Isaya uliyosema

Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai. "Yesu alitimiza unabii kwamba nabii Isaya aliongea na watu wa Israeli."

alichukua magonjwa yetu na kubeba malazi yetu

Mathayo anamnukuru nabii Isaya. Hii misemo miwili kiualisi inamaana moja na kusisitiza kwamba yeye aliponya magonjwa yetu yote. "aliponya wale walio wagonjwa na kuwafanya wazima."

Matthew 8:18

Sentensi unganisha

Hapa simulizi linabadilika na kusimulia jinsi Yesu alivyosema juu ya watu waliotaka kumfuata

Kisha

Hili neno limetumika hapa kuonyesha alama ya kikomo cha hadithi. Hapa Mathayo anaanza kueleza sehemu mpya ya hadithi.

yeye alitoa maelekezo

"aliwaambia wanafunzi wake"

Ndipo

Hapa inamaanisha baada ya Yesu "kutoa maelekezo" lakini kabla yake kuingia ndani ya boti.

popote

"sehemu yeyote"

Mbwea wana mashimo, na ndege wa angani wana vichari

Hii ina maana hata wanyama wakali wana sehemu ya kupumzika.

mbwea

Mbwea ni wanyama kama mbwa. Wanakula ndege wadogo na wanyama wengine wadogo. Ikiwa mbwea hawajulikani kwenye eneo lako, tumia kwa ujumla mbwa - kama viumbe au mnyama mwingine mkali.

shimo

Mbwea wanatengeneza mashimo ardhini kwa kuishi humo. Tumia neno sahihi kwa eneo ambalo mnyama "mbwea" anaishi.

mwanadamu

Yesu anaongelea kuhusu yeye mwenyewe

hana sehemu ya kulaza kichwa chake

Hii ina maanisha sehemu ya kulala. "hana sehemu yake ya kulala."

Matthew 8:21

niruhusu kwanza niende na kumzika baba yangu

Aieleweki kwamba baba wa mtu alikufa na angemzika mapema, au ikiwa mtu anaataka akae muda mrefu baba yake afe na amzike. Pointi ya muhimu mtu anataka kufanya kitu kingine kwanza kabla ya kumfuata Yesu.

uwaache wafu wazike wafu wenzao

Yesu hana maana halisi kwamba watu wafu watazika wafu wengine. Tafsiri inayowezekanaya "wafu" ni 1) ni msemo kwa wale ambao watakufa punde, au 2) ni msemo kwa wale ambao hawamfuati Yesu na kiroho wamekufa. Pinti ya muhimu ni kwamba wanafunzi wasiruhusu kitu chochote kumchelewesha kumfuata yesu.

Matthew 8:23

Sentensi unganishi

Hapa mandhari yanahamia kwenye simulizi la Yesu akituliza dhoruba wakati yeye na wanafunzi walipokuwa wakivuka bahari ya Galilaya.

alipoingia kwenye boti

"kuingia ndani ya boti"

wanafunzi wake wakamfuata

Jaribu kutumia neno lilelile kwa "wanafunzi" na "kufuata" ambalo umelitumia

Tazama

Hii inaonyesha kuanza kwa kutukio jingine kubwa la hadithi. Lugha yako inaweza ikawa na njia nyingine ya kuonyesha hili.

likatokea wimbi kubwa baharini

"wimbi la nguvu likatokea baharini"

ndipo sasa boti ikazungukwa na mawimbi

Hii inaweza kutafsiriwa kwa mfumo tendaji. "ndipo sasa mawimbi yakafunika boti"

wakamwamsha, wakamwambia,"tuokoe

Maana inayowezekana ni 1) kwanza walimwamsha Yesu na ndipo wakasema, "tuokoe" au 2) walipokuwa wakimwamsha walimwambia "tuokoe"

sisi

ikiwa unataka kutafsiri neno hili kama pamoja au kipekee, ndipo kipekee ni bora. Wanafunzi yawezekana walimaanisha walitaka Yesu awaokoe wanafunzi na yeye mwenyewe kwenye kuzama.

sisi tunaelekea kufa

"sisi tunakwenda kufa"

Matthew 8:26

wao

"kwa wanafunzi"

kwa nini mnaogopa ... imani?

Yesu alikuwa anakemea wanafunzi kwa swali la kejeli. "hampaswi kuogopa...imani" au "hamna sababu ya ninyi kuogopa ....imani."

ninyi wenye imani ndogo

Angalia jinsi unavyotafsiri hii

Huyu mtu niwa namna gani, kwamba hata upepo na bahari vinamtii yeye?

"Hata upepo na bahari vinamtii yeye! Huyu mtu ni wa namna gani?" Hili swali la kejeli linaonyesha kwamba wanafunzi walishangazwa. "huyu mtu niwa tofauti na hatujawahi kumwona! hata upepo na mawimbi vinamtii yeye!"

hata upepo na bahari vinamtii yeye

Kwa watu au wanyama kutii au kutotii haishangazi, lakini kwa upepo na maji inashangaza.Hii kibinadamu inaeleza vitu asili kama viumbe vinaweza kusikia na kuitikia kama watu.

Matthew 8:28

Sentensi unganishi

Hapa mwandishi anaturudisha kwenye wazo kuu la Yesu akiwaponyawatu. Hii inanzisha simulizi la Yesu akiwaponya wanaume wawili waliokuwa na pepo.

upande mwingine

"upande mwingine wa bahari ya galilaya"

nchi ya Gadalene

Gadalene ulitajwa kwa jina la Gadara.

walikuwa wasumbufu, hakuna mpita njia aliyeweza kupita njia ile

Mapepo yaliyowatawala watu hawa wawili yalikuwa hatari kwamba hakuna hata mmoja angeenda kupitia eneo hilo.

Tazama

Hii inaonyesha kuanza kwa kutukio jingine kubwa la hadithi. Inaweza kuhusisha watu tofauti na tukio lililopita, Lugha inaweza kuwa na njia ya kuonyesha hili.

Tuna nini cha kufanya nawe,mwana wa Mungu

Hili swali la kwanza la kejeli ni hostile

Umekuja hapa kututesa sisi kabla ya wakati kufika?

hili swali la pili la kejeli nalo pia ni uhasama na linamaanisha "Haupaswi kutomtii Mungu kwa kutuadhibu sisi kabla ya muda wenyewe ambao Mungu ameupanga ambao atuhukumu sisi"

Matthew 8:30

sasa

hili neno linaonyesha kwamba mwandishi atawaambia wasomaji habari anazotaka kufahamu kabla ya hadithi kuendelea. Nguruwe walikuwa kule kabla ya Yesu kufika.

Ikiwa utatuamuru tutoke

"kwa sababuunakwenda kututoa sisi nje"

sisi

Hii ni pamoja ,ina maanisha nguruwe pekee"

wao

mapepo ndani ya mtu

Mapepo wakawatoka na kwenda kwa nguruwe

"Mapepo wakamwacha mtu na kuwaingia nguruwe"

ndipo

Neno "ndipo" hapa linatoa angalizo kwetu kuwa tayari kwa taarifa za kushangaza zinazokuja.

likashuka chini kutokea mlimani

"kimbia haraka chini kwenye mteremko"

likafia majini

"waliingia kwenye maji na kuzama"

Matthew 8:33

Sentensi unganishi

Hii inahitimisha habari ya Yesu ya kuwaponya wanaume wawili waliokuwa na pepo

kuchunga nguruwe

"kulinda nguruwe"

kilitokea nini kwa mwanaume ambaye ametawaliwa na mapepo

"Yesu alifanya nini kwa mwanaume ambaye alitawaliwa na mapepo"

Ndipo

Hii inaonyesha mwanzo wa tukio jingine kubwa la hadithi. Inaweza kuhusisha watu tofauti na tukio la zamani.Lugha yako inaweza kuwa na njia kwa kuonyesha hili

mji mzima

Hii ina maanisha wengi au idadi ya watu wengi, sio lazima kila mtu.

mji

"jiji na ardhi inayoizunguka"

Matthew 9

Mathayo 09 Maelezo ya Jumla

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Kuna takwimu nyingi za matamshi katika sura hii. Ilikuwa ni kawaida pia kwa Yesu kutumia mifano ya analojia na sitiari katika mafundisho yake. Jinsi yake ya kufundisha ilikuwa na nia ya kukuza imani ndani yake. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Na", "lakini"

Baadhi ya tafsiri za Kiingereza huanzisha sentensi nyingi katika sura hii na neno "na" au "lakini" ili kuonyesha mfululizo wa matukio katika maelezo. ULB kawaida huondoa maneno haya kwa sababu muktadha wa hadithi yenyewe unaonyesha kuwa matukio hutokea kwa mfululizo. Inakubalika kutumia maneno haya ikiwa yana umuhimu katika tafsiri yako.

<< | >>

Matthew 9:1

Sentensi unganishi

Mwandishi anarejea kwenye wazo kuu, ambalo linaanzia 8:1, la Yesu akiwaponya watu. Hii inaanzisha habari ya Yesu akimponya mwanamume aliyekuwa amepooza

Yesu akaingia kwenye boti

Wanafunzi yamkini walienda na Yesu'

boti

Yamkini ni boti ile ile

akafika kwenye mji wake

"mji ambao yeye aliishi"

Ndipo

Hii inaonyesha mwanzo wa tukio jingine kubwa la hadithi. Linaweza kuhusisha watu wengine tofauti na tukio lililopita. Lugha yako inaweza kuwa na njia nyingine ya kuonyesha hili.

yao....zao

Hii inaonyesha wale ambao walimleta mgonjwa wa kupooza kwa Yesu. Hii inahusisha mgonjwa aliyepooza mwenyewe.

Mtoto

Huyu mtu hakuwa mtoto halisi wa Yesu. Yesu alikuwa akiongea naye kwa upole. Ikiwa hii inachanganya, inaweza pia kutafsiriwa"Rafiki yangu" au "Kijana" au hata kuondolewa.

Dhambi zako zimesamehewa

"Mungu amesamehe dhambi zako" au "Nimekusamehe dhambi zako"

Matthew 9:3

Tazama

Hii inaonyesha mwanzo wa tukio jingine kubwa la hadithi. Inaweza kutumia watu wengine tofauti na tukio lililopita. Lugha yako inaweza kuwa njia nyingine kufanya hili.

miongoni mwao

Hii inaweza kumaanisha "wao kwa wao,"kwenye mawazo yao, au "kwa kila mmoja," kutumia midomo yao.

anakufuru

Yesu alidai kuweza kufanya vitu ambavyo waandishi wa sheria walifikiri Mungu peke yake angevifanya.

akatambua mawazo yao

Yesu alitambua walichokuwa wakifikiria kwa uwezo wake au kwa sababu aliwaona wakisemezana wao kwa wao.

Kwa nini mnawaza maovu moyoni mwenu?

Yesu alitumia swali kuwakemea wanasheria.

wewe...yako

Hizi ni wingi

uovu

Huu ni uovu wa kimaadili au ukosefu, sio tu ni kosa kwa uhakika.

kipi ni rahisi......kutembea

Yesu aliuliza swali kukumbusha wanasheria kwamba waliamini mtu amepooza kwa sababu ya dhambi zake na kwamba dhambi zake zimesamehewa, naye angeweza kutembea, ili kwamba alipomponya aliyepooza, wanasheria wajue kwamba yeye anaweza kusamehe dhambi.

kipi kilicho rahisi kusema,dhambi zako zimesamehewa au kusema, simama na utembee?

"kipi ni rahisi kusema,"Dhambi zako zimesamehewa"? au ni rahisi kusema "Simamama na utembee"?

Dhambi zako zimesahewa

Hii inaweza kumaanisha 1)"ninakusamehe dhambi" au 2)"Mungu amesamehe dhambi zako."yako" ni umoja.

mtambue ya kwamba

"Nitawahakikishia ninyi." "ninyi" ni wingi.

yako.....yako

Hizi ni umoja

nenda nyumbani kwako

Yesu hamkatazi mtu kwenda sehemu nyingine. Yeye anampa fursa ya kwenda nyumbani.

Matthew 9:7

Sentensi unganishi

Hii inahitimisha habari ya Yesu ya kumponya mtu aliyepooza. Kisha Yesu akamwita mtoza ushuru kuawa mmoja wa wanafunzi wake.

ambaye amewapa

"kwa sababu amewapa"

mamlaka hayo

mamlaka ya kuthibitisha kusamehe dhambi

Na Yesu alipokuwa akipita kutoka hapo

Kirai hiki kinaonyesha mwanzo wa simulizi mpya. Kamalugha yako ina namna ya kufanya hili, unaweza kulitumia mahali hapa.

akaipita kutoka hapo

"alikuwa akiondoka" au "alikuwa akienda"

Mathayo...naye...Yeye

Utamaduni wa kanisa unasema Mathayo ni mwandishi wa hii Injili, lakini andiko halitoi sababu ya kubadilisha kiwakilishi kutoka "naye" na "yeye" kwa "kwangu" na "mimi"

Yeye alisema naye

"Yesu alisema na Mathayo"

naye akamwambia

"Yesu alimwambia Mathayo"

Naye akasimama na kumfuata yeye

"Mathayo alisimama na kumfuata yeye" kama mwanafunzi, siyo tu kujumuika na Yesu kwa kinachofuata kukamilisha.

Matthew 9:10

Maelezo kwa ujumla

Matukio haya yalitokea kwenye nyumba ya Mathayo mtoza ushuru

nyumba

Hii yawezekana ni nyumba ya Mathayo, lakini yawezekana kuwa nyumba ya Yesu(walitumia kula Yesu na wanafunzi wake")Kilitengwa maalum ikiwa kitahitajika kuepusha kuchanganywa.

Ndipo

Hii inaonyesha mwanzo wa tukio jingine katika habari kuu. Inaweza kuhusisha watu tofauti kuliko matukio yale ya kwanza. Lugha yako inaweza kuwa na namna ya kulielezea hili.

Mafarisayo walipoona hayo

"Na mafarisayo walipoona kwamba Yesu alikuwa anakula na watoza ushuru na watu wenye dhambi"

kwa nini mwalimu wenu anakula pamoja na watoza ushuru na waovu?

Mafarisayo walitumia swali hili kumkosoa Yesu kile alichokuwa akifanya.

Matthew 9:12

Maelezo y a jumla

Matukio haya yanatokea kwenye nyumba ya Mathayo mtoza ushuru.

Na Yesu aliposikia hayo

Hapa "hayo" inarejea swali ambalo mafarisayo waliuliza kuhusu Yesu kula na watoza ushuru na wenye dhambi.

Watu walio na afya nzuri hawahitaji mganga, isipokuwa wale walio wagonjwa

Yesu anajibu kwa kutumia mithali. Anamaanisha kuwa anakula na watu wa aina hii kwa sababu amekuja kuwaokoa wenye dhambi.

watu walio na afy nzuri

"watu wenye afya"

wale walio wagonjwa

Kirai "wanahitaji mganga" kinaeleweka. "Wagonjwa ndio wanaohitaji mganga"

Inawapasa muende mukajifunze maana yake

Yesu anaelekea kunukuu maandiko. "Inakupasa ujifunze maana ya kile ambacho Mungu alisema katika maandiko"

Inawapasa muende

Kiwakilishi "wa" ni cha wingi kinachomaanisha mafarisayo

Ninapenda rehema na wala siyo dhabihu

Yesu ananukuu kile ambacho nabii Hosea aliandika katika maandiko.. Hapa "Ni" inamaanisha Mungu.

Kwa kuwa nilikuja

Hapa "Ni" inamaanisha Yesu.

haki

Yesu anatumia kejeli. Hadhani kuwa kuna watu wenye haki ambao hawahitaji kutubu. "wale wanaodhani kuwa ni wenye haki"

Matthew 9:14

sentensi unganishi

Wanafunzi wa Yohana mbatizaji walihoji swala la wanafunzi wa Yesu kutokufunga.

msifunge

"endeleeni kula kama kawaida"

Je wasindikizaji wa arusi wanaweza kuwa na huzuni pindi bwana harusi anapokuwa pamoja nao?

Yesu anatumia swali kuwajibu wanafunzi wa Yohana. Walijua kuwa watu hawaombolezi na kufunga kwenye sherehe ya harusi. Yesu anatumia mithali hii kuonyesha kuwa wanafunzi wake hawaombolezi kwa sababu yeye bado yuko nao.

Lakini siku zinakuja

"lakini muda utafika"

bwana arusi atachukuliwa kutoka kwao

Hii inaweza kuelezeka katka mfumo tendaji. "Bwana harusi hatakuwa pamoja nao si muda mrefu ujao" au "kuna mmoja atakayemchukua bwana harusi kutoka kwao."

atachukuliwa kutoka kwao

Yamkini Yesu anamaanisha kifo chake, lakini hii isiwekwe wazi kuwa ndichio alichomaanisha. Ili kulinda picha ya harusi, ni vizuri kueleza kuwa bwana harusi ataondoka kitambo.

Matthew 9:16

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kujibu swali ambalo wanafunzi wa Yohana walikuwa wameuliza

Hakuna anayeweka kipande cha nguo mpya kwenye nguo ya zamani

Huu msemo una maana kwamba watu wanaojua utamaduni wa zamani pekee hawako tayari kukubali mpya.

vazi

nguo

kipande

"kipande cha nguo mpya" kinatumika kuziba nguo iliyochanika

na mpasuko mkubwa utatokea

Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji

Matthew 9:17

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kujibu swali ambalo wanafaunzi wa Yohana walikuwa wameuliza

Hakuna watu wanaoweka mvinyo mpya katika ngozi ya zamani

Yesu anatumia mithali Nyingine kuwajibu wanafunzi wa Yohana. Hii inamaanisha ni kitu kilekile sawa na mithali ya 9:16

Hakuna watu wanaoweka

"Hakuna hata mmoja anayemwaga" au "Watu hawaweki kamwe"

mvinyo mpya

Huu ni mvinyo ambao haujachacha. Kama mizabibu haijulikani kwenye sehemu yenu, tumia neno la ujumla la tunda."mvinyo wa matunda"

mfuko wa mvinyo mkuukuu

Hii inamaanisha mifuko ya mvinyo ambayo imekuwa ikitumika mara nyingi.

Mfuko wa mvinyo

"mkoba wa mvinyo" au "mkoba wa ngozi". Hii ni mifuko iliyokuwa imetengenezwa kwa ngozi za wanyama.

mvinyo utatoweka na gozi itaharibika

Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji. "Na hii itaharibu mfuko wa mvinyo na mvinyo kumwagika.

ngozi itaharibika

mvinyo mpya unapochacha na kuumuka, ile ngozi huchanika kwa sababu haiwezi tena kutanuka.

ngozi mpya

"mifuko mipya ya mvinyo" au "begi jipya la mvinyo" Hii inamaanisha ngozi ya mvinyo ambayo haijawahi kutumika.

vyote vitakuwa salama

Hili linaweza kuelezwa kwa mfumo tendaji

Matthew 9:18

Sentensi unganishi

Hii inaanzisha simulizi ya Yesu kumfufua binti wa afisa wa Kiyahudi baada ya kufa.

mambo hayo

Hii inarejea jibu la Yesu alilowapa wanafunzi wa yohana kuhusu kufunga.

Tazama

Neno "tazama" linatupa dokezo la mtu mwingine mpya katika hadithi. Lugha yako inawezekana ikawa na njia nyingine ya kufanya hivi.

akasujudu kwake

Hii ni njia mtu yeyote kuonyesha heshima katika utamaduni wa kiyahudi.

njoo na uweke mkono wako juu yake, na yeye ataishi tena

Hii inaonyesha kwamba ofisa wa kiyahudi aliamini Yesu ana nguvu ya kurudisha uhai wa binti yake.

wanafunzi wake

wanafunzi wa Yesu

Matthew 9:20

Sentensi unganishi

Hii inafafanua jinsi Yesu alivyomponya mwanamke mwingine wakati akiwa njiani kwenda kwa afisa wa Kiyahudi

Tazama

Neno "tazama" linadokeza juu ya mtu mwingine katika hadithi. Lugha yenu inaweza kuwa na njia nyingine ya kufanya hivi

alikuwa anatokwa damu

"kutokwa damu mfululizo"Yawezekana alikuwa akitokwa damu kwenye tumbo lake ingawa haikuwa kipindi cha kawaida yake. Baadhi ya tamaduni yawezekana wana namna nzuri ya kueleza tatizo hili.

miaka kumi na mbili

"miaka 12"

vazi

"kanzu"

Endapo nitagusa vazi lake, nami nitapata uponyaji

Alifikiria hivi kabla hajamgusa Yesu. Unaweza kuiweka sentensi hii mwanzoni.

Endapo nitagusa vazi lake

Kwa mjibu wa sheria za Kiyahudi, kwa sababu ya kutokwa na damu hakutakiwa kumgusa yeyote mtu yeyote. Anagusa vazi la Yesu ili nguvu za Yesu zimponye alidhani kuwa Yesu hatagundua kuwa ameguswa

Lakini

"Badala" Kile mwanamke alichotumaini kutokea hakikutokea.

Binti

Mwanamke hakuwa mtoto halisi wa Yesu. Yesu alikuwa akiongea naye kwa upole. Ikiwa hii inachanganya, inaweza kutafsiriwa "kijana wa kike" au hata kutolewa.

imani yako imekufanya upone

"Kwa sababu uliniamini, Nitakuponya"

Muda huo huo mwanamke alipokea uponyaji

Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo tendaji. "Yesu alimponya hapohapo"

Matthew 9:23

Sentensi unganishi

Hii inarudisha habari ya Yesu kumfufua binti wa afisa wa Kiyahudi

nyumba ya ofisa

Hii ilikuwa nyumba ya kiongozi wa kiyahudi

wapiga tarumbeta na umati wa watu walikuwa wakipiga kelele

Huu ni utamaduni wa kawaida wa kumboleza pale mtu anapokuwa amekufa.

wapiga zumari

"watu ambao wanapiga zumari/filimbi"

Ondoka hapa

Yesu alikuwa akiongea kwa watu wengi, hivyo tumia mfumo wa wingi wa kutoa amri kama lugha yenu inao huo.

binti hajafa, lakini amelala

Yesu anatumia igizo la maneno. Ilikuwa ni kawaida kipindi cha Yesu kusema mtu aliyekufa kuwa "amelala" Lakini hapa binti aliyekufa ataamka, ingawa yeye alikuwa amelala.

Matthew 9:25

Sentensi unganishi

Hii inahitimisha simulizi la Yesu la kumfufua binti wa afisa wa Kiyahudi

Maelezo kwa ujumla

Mstari wa 26 unatoa muhtasari unaofafanua matokeo ya Yesu kumfufua huyu msichana.

Na wale watu walipotolewa nje

"Baada ya yesu kuwatoa watu nje" au "Baada ya familia kuwatoa watu nje"

akaamka

"akaamka kutoka kitandani" Hii ni maana ile ile kama iliyo kwenye 8:14

Habari hii ikaenea mji mzima

Watu wote wa mji ule walisikia kuhusu hilo" au "Watu walioona binti akiwa hai walianza kuwaambia watu wa eneo hilo habari hizi."

Matthew 9:27

Sentensi unganishi

Hii inaanzisha habari ya Yesu akiwaponya wanaume wawili waliokuwa vipofu

Alipokuwa akipita Yesu njiani

Yesu alikuwa akiondoka kwenye mji

akipita

"Alikuwa akiondoka" au "alikuwa akienda"

wakamfuata

Hii inamaainisha kuwa walikuwa wakitembea nyuma ya Yesu, siyo lazima kuwa walikuwa wameshakuwa wanafunzi wake.

uturehemu

Inamaanisha kuwa walitaka Yesu awaponye

Mwana wa Daudi

Yesu hakuwa mwana halisi wa Daudi, hivyo inaweza kutafsiriwa kama "Ukoo wa Daudi". Ingawa, "Mwana wa Daudi" pia ni cheo alichopewa Masihi, na wale wanaume yawezekana walikuwa wakimwita Yesu kwa Sifa hii.

Pindi Yesu alipokuwa amefika kwenye nyumba

Hii inaweza kuwa nyumba ya Yesu au nyumba iliyosemwa kwenye 9:10

Ndiyo,Bwana

Jibulote halijatolewa lakini linaeleweka "Ndiyo, Bwana, tunaamini kuwa unaweza kutuponya."

Matthew 9:29

akagusa macho yao na kusema

Haiko wazi kuwa aligusa macho yao wote wakati mmoja au alitumia mkono wake wa kulia kumgusa mmoja na mwingine tena. Mkono wa kushoto kawaida ulitumika kwa makusudi yakutokuwa safi, ni hakika alitumia mkono wa kulia pekee. Pia haiko wazi kwamba aliongea wakati anawagusa au kwanza aliwagusa na ndipo akaongea kwao.

Na ifanyike hivyo kwenu kama imani yenu ilivyo

Hii inaweza kutafsriwa katika mfumo tendaji. "Naitafanya kama ulivyomini" au "kwa sababu unaamini, nitakupaonya"

macho yao yakafumbuka

Hii inamaanisha waliweza kuona. Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo tendaji. "Mungu aliponya macho yao" au "wale wanaume wawili vipofu waliweza kuona"

Angalieni mtu yeyote asifahamu jambo hili.

Hapa neno "angalieni" linamaanisha "hakikisha." au "Uwe na Muwe na uhakika hakuna mtu atakaye tafuta juu ya jambo hili" au "Msimwambie mtu yeyeote kuwa nimewaponya"

Lakini

"Badala yake"Wanaume hawakufanya kile ambacho Yesu aliwaambia kufanya.

kutangaza habari

"waliwaambia watu wengi kilichotokea kwao"

Matthew 9:32

Sentensi usganishi

Hii ni habari ya Yesu akiwaponya watu waliokuwa wamepagawa na pepo

tazama

Neno "tazama" linadokeza sisi juu ya mtu mwingine katika simulizi. Lugha yako inaweza ikawa njia nyingine ya kufanya hizi.

mtu mmoja bubu ... akaletwa kwa Yesu.

Hii inaweza kuelezeka kwa muundo tendaji. "mtu mmoja alimleta bubu kwa Yesu... kwa Yesu"

bubu

asiyeweza kuongea

aliyepagawa na pepo

Hii inaweza kueleza katika mfumo tendaji. "ambaye pepo lilikuwa limemumliki" au "amabye pepo lilikuwa linamtawala"

Na pepo walipomtoka

Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji. "Baada ya Yesu kuwa amelitoa pepo" au " Baada ya Yesu kuwa ameliamuru pepo kutoka"

yule bubu aliongea

"Yule bubu akanza kuongea" au "yule aliyekuwa bubu aliongea" au "mtu ambaye alikuwa bubu akaongea" au yule mtu hakuwa bubu tena"

umati ukashangazwa

"Watu walishangazwa"

Hii haijawahi kutokea

Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji "Hii haikuwahi kutokea kabla" au "Hakuna hata mmoja aliyewahi kufanya jambo kama hili hapo awali."

anawafukuza pepo

"huwalazimisha pepo kutoka"

huwaondoa

Kiwakilishi "ana" kinamaanisha Yesu

Matthew 9:35

Sentensi unganishi

Mstariwa 35 ni mwisho wa sehemu ya simulizi ambayo imeamnzia katika 8:1 kuhusu huduma ya Yesu ya uponyaji kule Galilaya.

Maelezo kwa ujumla

Mstari wa3 6 unaanzisha sehemu nyingine ya simulizi ambapo Yesu anawafundisha wanafunzi wake na kuwatuma kwenda kuhubiri na kuponya kama alivyokuwa akifanya.

miji yote

Yesu alienda kwa wengi au kwa miji mingi lakini si kwa kila mji. "Katika miji mingi"

miji....vijiji

"vijiji vikubwa...vijiji vidogo" au "miji mikubwa...miji midogo"

injili ya ufalme

Hapa neno "Ufalme" linamaanisha utawala wa Mungu kama mfalme. tazama ilivyotafsiriwa karika 4:23

magonjwa ya kila aina na udhaifu wa aina zote

"kila magonjwa na kila udhaifu" Neno "magonjwa" na "udhaifu" yanakaribiana kufanana lakini yanapaswa kutafsiliwa tofauti kama inawezekana. "Ugonjwa" unamfanya mtu kuwa dhaifu. "Udhaifu" kukosa nguvu mwili au tokeo linalosababishwa na kuwa na ugonjwa.

Walikuwa kama kondoo wasio na mchungaji

Mfanano huu unamaanisha kuwa hawakuwa na kiongozi wa kuwaangalia. "Watu hawakuwa na kiongozi"

Matthew 9:37

Maelezo kwa ujumla

Yesu anatumia mithali kuwaambia wanafunzi wake juu ya mavuno ili kuona jinsi watavyopokea mahitaji ya makutano yaliyotajwa katika sehemu ambazo tayari zimepita.

Mavuno ni mengi, lakini wafanyakazi ni wachache

Yesu anatumia mithali kuonyesha jinsi anavyopokea kile anachokiona. Yesu anamaanisha kuwa kuna watu wengi walio tayari kumwani Mungu lakini kuna watu wachache tu wa kuwafundisha ukweli wa Mungu.

mavuno ni mengi

"Kuna mazao mengi yaliyoiva na yako tayari kuvunwa."

wafanya kazi

"watendaji"

mwombeni Bwana wa mavuno

"Mwombeni Bwana, kwa sababu yeye mkuu wa mavuno"

Matthew 10

Mathayo 10 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Kutumwa kwa wanafunzi kumi na wawili

Sehemu kubwa ya sura hii inazungumza juu ya Yesu kuwatuma wanafunzi kumi na wawili kutoa ujumbe wake kuhusu ufalme wa mbinguni. Walipaswa kufanya huduma yao kwa inchi ya Israeli pekee na wasije wakashiriki habari hii kwa wasio Wayahudi. Maagizo ya Yesu humpa msomaji hisia kwamba hawakupaswa kupoteza wakati wowote. Sauti yake iliashiria kuwa alitaka waharakishe.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Wanafunzi kumi na wawili

Yafuatayo ni orodha ya wanafunzi kumi na wawili: Katika Mathayo: Simoni (Petro), Andrea, Yakobo mwana wa Zebedayo, Yohana mwana wa Zebedayo, Filipo, Bartholomayo, Tomasi, Mathayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mzeloti na Yuda Iskarioti.

Katika Marko: Simoni (Petro), Andrea, Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana mwana wa Zebedayo (ambaye aliwaita Boanerge, yaani, wana wa ngurumo), Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomasi, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mzeloti, na Yuda Iskarioti.

Katika Luka: Simoni (Petro), Andrea, Yakobo, Yohana, Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomasi, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni (aitwaye Mzeloti, Yuda mwana wa Yakobo, na Yuda "Iskarioti.

Inawezekana kuwa Thadayo na Yuda, mwana wa Yakobo, ni majina mawili ya mtu mmoja.

"Ufalme wa mbinguni umekaribia"

Maneno haya yana umuhimu mkubwa wa kitheolojia. Wataalam wanajadili ikiwa "ufalme wa mbinguni" ulikuwepo wakati huu au bado unakuja. Tafsiri za Kiingereza mara nyingi hutumia maneno "karibu," lakini hii inaweza kusababisha changamoto katika kutafsiri. Matoleo mengine hutumia maneno "inakaribia" na "yamekaribia."

<< | >>

Matthew 10:1

Sentensi unganishi

Hii inafungua habari ya Yesu akiwatuma wanafunzi wake wakafanye kazi yake.

akawaita wanafunzi wake kumi na wawili pamoja

"Akawaelezea wanafunzi wake 12"

akawapa mamlaka

Uwe na uhakika kwamba ujumbe unakuwa wazi kuwasilisha kwamba haya mamlaka yalikuwa 1) ni kufukuza roho chafu na 2) kuponya magonjwa na udhaifu

kuwafukuza

"kuwafanya roho wachafu waondoke"

kila aina ya magonjwa na kila aina za udhaifu

"kila ugonjwa na kila udhaifu." Maneno "ugojwa" na "udhaifu" ni kama yanakaribia kufanana lakini yanapaswa kutafsiliwa tofauti kama inawezekana. "Ugonjwa" ni kisababishi cha mtu kuwa dhaifu. "Udhaifu" ni ukosefu wa nguvu mwilini au kisababishi ambacho matokeo yake ni kuwa na ugonjwa.

Matthew 10:2

Maelezo kwa ujumla

Hapa mwanadishi anatoa majina kumi na mbili ya mitume kama taarifa ya itoayo picha ya nyuma.

sasa

Neno hili limetumika hapa kuonesha mwanzo wa simulizi jipya. Hapa Mathayo anaonesha historia ya maisha ya mitume kumi na wawili.

Mitume kumi na wawili

Hili kundi ni sawa na kusema "wanafunzi kumi na wawili" katka 10:1

Kwanza

Hi ya kwanza kwa mpangilio si kwa safu

Mkananayo

Hii inaweza kumaanisha yafuatayo 1) "Mkananayo" hii ni sifa iliyoonesha kuwa alikuwa ni mshirika wa kundi lililotaka kuwaweke huru wayahudi kutoka kwenye utawala wa Warumi. "Mzalendo" au "mmajumui" au 2) Mkereketwa ni neno linalonesha mtu mwenye kutamani kumjengea heshima Muungu. "mwenye uchu"

Mathayo mtoza ushuru

"Mathayo ambaye alikuwa mtoza ushuru"

ambaye atamsaliti yeye

"ambaye atamsaliti Yesu"

Matthew 10:5

Sentensi unganishi

Hapa Yesu anaanza kutoa maelekezo kwa wanafunzi wake juu ya jinsi wanavyopaswa kufanya na wategemee nini wakienda kuhubiri.

Maelezo kwa ujumla

Ijapokuwa mstari wa tano unaanza kwa kusema kuwa alaiwatuma thenashara, Yesualiwapa maelekezo haya kabla ya kuwatuma.

Hawa kumi na wawili Yesu aliwatuma

"Yesu aliwatuma hawa wanaume kumi na wawili" au "Walikuwa ni hawa wanaume kumi na wawili ambao Yesu aliwatuma"

aliwatuma

Yesu aliwatuma kwa kusudi maalumu.

Naye akawaelekeza wao

"Naye aliwaambia kitu gani walipaswa kutenda" au "aliwaamuru wao"

Kondoo aliyepotea wa nyumba ya Israel

Hiki ni kirai kinacholinganisha taifa zima la israel na kondoo ambao wamejitenga kutoka kwa mchungaji

nyumba ya Israel

Haya maelezo yana maanisha taifa la Israel. "watu wa Israel" au "kizazi cha Israel"

Mnapokwenda

Kiwakilishi "mna" ni cha wingi na kinamaanisha mitume kumi na wawili.

Ufalme wa mbinguni umekaribia

Hiki kirai cha "ufalme wa mbinguni", kinapatikana katika injili ya Mathayo tu. Kinamaanisha Mungu ni mfalalme. kama inawezekana tumia neno "mbinguni" katikatafsiri zako. "Mungu wetu wa mbinguni atajidhihirisha mapema kuw a yeyeni mfalme. Tazama ilivyotafsiriwa katika 3:1

Matthew 10:8

Sentensi unganishi

Yesu anaendele kuwaelekeza wanafunzi wake mambo ya kufanya watakapoenda kuhubiri.

mme....zenu

Hivi ni viwakilishi vya wingi vinavyomaanisha mitume kumi na wawili

Mmepokea bure toeni bure

kuna taarifa hapa ambazo hazikuelezwa, lakini inaeleweka . " Nilwasaidia na kuwafundisheni neno la Mungu bure. Kwa hiyo msiwafanye watu wengine wawalipe kwa lengo la kuwasaidia au kuwafundisha ukweli wa Munugu.

dhahabu,fedha au shaba

Hizi ni metali ambazo zilitumika kutengeneza sarafu. Hii orodha ni ya hela, ikiwa metali hazijulikani katika eneo lako, tafasiri orodha kama"hela."

pochi

Hii ina maana "mkanda" au "mkanda wa fedha," lakini kinamaanisha chochote kinachotumika kubebea hela. Mkanda ni kitu kirefu cha kujifunga cha nguo au ngozi kinachopita begani. Kilikuwa ni kipana ambacho kiliweza kukunjwa na kutumiwa kubeba hela

begi la kusafiria

Hii inaweza kuwa begi lolote linalotumika kubeba kitu safarini au begi linalotumiwa na mtu mmoja kukusanya chakula au hela.

nguo ya ziada

Tumia neno hilo hilo ulilotumia kwa "nguo"

mfanyakazi

"mfanyakazi"

chakula chake

Hapa "chakula" Kitu chochote ambacho ni hitaji kwa mtu.

Matthew 10:11

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwaelekeza wanafunzi wake kuhusu nini wanachopaswa kufanya watakapoenda kuhubiri.

mta...yenu

Hivi viwakilishi vinaonyesha mitume kumi na wawili

Kwa kila mji au kijiji mtakachoingia

"Kwa "Kila mji au kijiji" mtakachokwenda" au

Mji..kijiji

"kijiji kikubwa...kijiji kidogo" au "mji mkubwa...mji mdogo." Tazama ilivyotafsriwa katika 9:35.

anayestahili ... asiyestahili

Katika 10:11-13 "anayestahili" inamaanisha mtu aliyetayari kuwakaribisha wanafunzi wa Yesu. Yesu anamlinganisha mtu asiyekuwa tayari kuwakaribisha wanafunzi wake saw namtu asiyestahili

mkae pale mpaka mtakapoondoka

Maana halisi ya sentensi hii inaweza kuwa sahihi kama itasemwa "mkae katika nyumba ya huyo mtu mpaka mtakapoondoka kwenye huo mji au kijiji"

Mtakapoingia katika nyumba,salimuni

Kirai cha "salimieni" inamaanisha isalimuni hiyo nyumba. Salamu ya kawaida kwa nyakati zile ilikuwa "amani iwe katika nyumba hii. "Kaya" inamaanisha watu wanao ishi kwenye hiyo nyumba. mkiwa mnaingia kwenye nyumba, muwasalimu watu wanaoishi ndani yake.

nyumba inastahili

"Nyumba" inamaanisha wale wanaoishi kwenye hiyo nyumba. "watu wanaoishi kwenye nyumba hiyo wakiwakaribisha vizuri" au kaya ile iwakiwakarimu vizuri"

amani yenu ibaki pale

Neno "pale" linamaanisha kaya. Nyumba hapa inamaanisha watu wanaoishi kwenye hiyo nyunba. Amani yenu ibaki pale" au "watu wanaoishi katika nyumba ile wataishi katika amani"

amani yenu

Hii ni amani ambayo mitume wanapaswa kumwomba Mungu awape wanaoishi katika nyumba.

Kama haistahili

Neno "pale" linamaanisha nyumba . "Nyumba" inamaanisha kaya. "ikiwa hawatawakaribisha vizuri" au ikiwa hawatawakarimu"

amani yenu iondoke pamoja nanyi

Yamkini ina maana zifuatazo: 1) Ikiwa nyumba haistahili, ndipo Mungu atazuia amani au baraka katika nyumba hiyo au 2) Ikiwa kaya haistahili, ndipo mitume walipaswa kufanya kitu, kama vile kumwomba Mungu asikubali heshima ya salaam za amani. Ikiwa lugha yako ina maana kama hii ya kurudisha salaam au matokeo, hivyo itumike hapa.

Matthew 10:14

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwaelekeza wanafunzi wake cha kufanya watakapoenda kuhubiri

Na kwa wale wasiowapokea au kusikiliza

"Ikiwa hakuna watu watakaowakaribisha au kuwasikia katika mji huo"

ninyi ... yenu

Hivi ni viwakilishi vya wingi ambavyo vinamaanisha mitume kumi na mbili

kusikiliza maneno yenu

Hapa "maneno" inamaanisjha kile ambacho wanafunzi wa Yesu watasema. "kusikiliza ujumbe wenu" au "kusikiliza kile mnachotaka kusema"

mji

Unaweza kutafsiri kama ulivyofanya kwa njia hiyo hiyo

jipanguseni mavumbi ya mguuni

"jipanguseni mavumbi y a miguu yenu mnapoondoka." Hii ni ishara inayoonesha kuwa Mungu amaewakataa watu wa mji au nyumba hiyo.

kweli nawaambia

"Nawaambia ukweli." Kirai hiki kinaongeza msisitizo kwa kile ambacho Yesu atasema baadaye.

itakuwa zaidi ya kuvumilia

"mateso yatakuwa machache"

mji wa Sodoma na Gomora

Hii inamaanisha watu walioishi Sodoma na Gomora."watu ambao waliishi katika miji ya Sodoma na Gomora"

mji huo

Hii inamaanisha watu katika mji ambao hawakutaka kuwapokea mitume au kusikiliza ujumbe wao. "Watu wa mji huo ambao hawakuwapokea"

Matthew 10:16

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwaelekeza wanafunzi wake. Hapa anaanza kuwaambia wao kuhusu dhiki ambayo wanatakiwa kuvumilia pindi watapoenda kuhubiri.

Angalia

Neno "Angalia" hapa linaongeza na kusisitiza ambacho kitafuatia. "Tazama"au "Sikiliza" au "Zingatia kile ninachotaka kukuambia"

Ninawatuma

Yesu anawatuma kwa kusudi maalum.

kama kondoo katikati ya mbwa mwitu

Kondoo ni wanyama wasioweza kuijhami ambao mara kwa mara hushambuliwa na mbwa mwitu. Yesu anasema kuwa watu wanaweza kuwaumiza wanafunzi wake. "Kama kondoo katikati ya mbwa mwitu hatari" au "kama kondoo katikati ya watu wenye tabia kama hizo.

muwe na hekima kama nyoka na wapole kama njiwa

Yesu awaambia wanafunzi wake ili wawe na tahadhari na wasiowamiza watu. Kama kuwafananisha wanafunzi na nyoka au na njiwa kunachanganya, basi ni vizuri kutokuutumia huu mlinganyo. "fanya kwa kuelewa na tahadhari, vile vile kwa makini na wema."

Muwe waangalifu na watu watawapeleka

Unaweza kutafsiri kwa kutumia "kwa sababu" ili kuonnesha jinsi hizi sentensi zinavyohusiana. "Muwe waangalifu na watu kwa sababu watawapeleka

Watawapeleka kwenye

"watawasaliti kwa" au "watawakabidhi Kwa" au watawakamata na kuawajaribu"

mabaraza

"mahakama" Hawa ni viongozi wa kidini au wazee ambao kwa pamoja wanalinda amani katika jamii.

watawapiga mijeledi

"kupiga kwa mijeledi"

katikati ya mbwa mwitu

AT:"katikati ya watu ambao ni kama mbwa mwitu wa hatari" au "katikati ya watu ambao watenda kama wanyama wa kutisha" au "katikati ya watu ambao watakuvamia wew"

na mtaletwa

Hii inaweza kuelezeka katika muundo tendaji "watawaleta" au "watawaburuza"

kwa ajili yangu

"kwasababu ninyi ni wangu" au "kwa sababu mnanifuata mimi"

kwao na kwa mataifa

Kiwakilishi "kwao" inamaanisha huenda wakawa "magavana au wafalme" au kwa washitaki wa kiyahudi

Matthew 10:19

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwaelekeza wanafunzi wake kuhusu dhiki wanayotakiwa kuvumilia pindi watapoenda kuhubiri

msi...yenu

kiwakilishi "msi" na "yenu" vinamaanisha mitume kumi na wawili

msiwe na wasiwasi

"msiwe na hofu"

jinsi gani au nini cha kuongea

"jinsi gani ya kuongea au nini cha kusema." Haya mawazo mawili yanaweza kujumuishwa:"Ni nini cha kusema"

kwa kuwa kitu cha kusema mtapewa

Hii inaweza kutafsirika katika mfumo tendaji. "Kwa kuwa Roho mtakatifu atawapa cha kusema"

kwa wakati huo

Hapa wakati" unamaanisha "muda huohuo" au "kwa muda huo"

Pindi watakapowashutumu

Kipindi watu watakapowashitaki kwenye mabaraza.""watu" hapa ni wale wale "watu"

Roho ya Mungu wako

Ikiwa muhimu, inaweza kutafsiliwa kama "Roho ya Mungu baba yako aliye mbinguni" au nyongeza inaweza kuongezwa ili kufafanua kwamba inamaanisha Roho ya Mungu baba na sio roho ya baba wa ulimwengu.

Baba

Hii ni sifa muhimu ya Mungu.

Ndani yako

"kupitia ninyi"

Matthew 10:21

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwaelekeza wanafunzi wake kuhusu dhiki wanayotikiwa kuvumilia pindi watakapoenda kuhubiri

Ndugu atamwinukia ndugu yake kumwua, na baba kwa mtoto wake

Kirai hiki cha "baba na mtoto wake" kinawza kutafsiriwa kama sentensi timilifumilifu. Ndugu atamwinukia ndugu na kumwua, na baba atamwinukia mtoto wake na kumwua"

kumwinukia

"saliti" au "kumtoa" Tazama ilivyotafsiriwa kwenye 10:6

kifo

Nomino dhania "kifo" inaweza kutafsiriwa uthabiti, kwa uwazi zaidi. "mahakamani il mamlaka iweze kuwahumu

kumwinukia dhidi ya

"kupigana dhidi" au "kwenda kinyume dhidi ya"

na kusababisha kuingia katika kifo

Hii inaweza kutafsiriwa katika mfumo tendaji. "na kuwaweka katika kifo" au "na wenye mamlaka kuwaweka katika kifo"

Nanyi mtachukiwa na kila mtu

Hii inaweza kutafsirika katika muundo tendaji. "Kila mtu atawachukia" au "Watu wote watawachukia ninyi"

nanyi

Hiki ni kiwakilishi cha wingi kichonamaanisha mitume kumi na mbili.

kwa sababu ya jina langu

Hapa "jina" inamaanisha ukamilfu wa nafsi "kwa sababu yangu" au "kwa sababu mlinitumaini mimi"

yeyote atakayevumilia

" atakayebaki kuwa mwaminif."u

mtu huyo ataokolewa

"yeyote atakayekuwa mwaminifu"

mji huu

Neno "hapa" halina maana ya mji maalumu. "mji mmoja"

kimbilieni mji unaofuata

"mwende mji unaofuata"

Kwa kweli nawaambia

"Nawaambia ukweli." Kirai hiki kinaongeza msisitizo wa kile ambacho Yesu atasema baadaye.

Mwana wa Adamu

Yesu anaongea juu yake mwenyewe

amekuja

"amewasili"

Matthew 10:24

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwaelekeza wanafunzi wake kuhusu dhiki wanayotakiwa kuvumilia wakati watakapoenda kuhubiri.

Mwanafunzi si mkuu kuliko mwalimu wake, wala mtumwa aliye juu ya bwana wake

Yesu anatumia mithali kuwafundisha wanafunzi wake ukweli wa jumla. Yesu anasisitiza kwamba wanafunzi wake wasitegeme watu kuwatendea vizuri kuliko walivyomtendea Yesu.

Mwanafunzi si mkuu kuliko mwanafunzi wake

"Mwanafunzi daima si wa mhimu kuliko mwalimu wake". Mwalimu daima ni wa mhimu kuliko mwanafunzi wake.

wala mtumwa aliye juu ya bwana wake

"na mtumwa daima si wa mhimu kuliko bwana wake" au "na bwana daima ni wa muhimu kuliko mtumwa wake"

Inatosha kwa mwanfunzi kwamba awe kama mwalimu wake

"Mwanafunzi atalizika pale atakapokuwa kama mwalimu wake"

awe kama mwalimu wake

Kama inawezekana, unaweza kueleza dhahIri jinsi mwanafunzi anavyofanyika kuwa kama mwalimu, "Ajue kma mwalimu anavyojua"

na mtumwa kama bwana wake

Kama inawezekana uieleze dhahiri jinsi mtumwa anvyoweza kuwa kama bwana ." "na mtumishi atarizika pale tu atakapokuwa na umuhimu kama Bwana wake"

Ikiwa wamwita bwana ... wa nyumba Belzabuli, ni kwa kiasi gani zaidi kwa wale wa nyumba yake

Kwa mara nyingine Yesu anasisitiza kuwa kama watu walimtenda vibaya, hivyo wanafunzi wategemee kufanyiwa hivyo au zaidi.'

ni kwa kiasi gani watawakashifu watu wa nyumba yake

" majina yale wanayotumia kuwaita watu wa nyumba yake hakika yatakuwa mabaya zaidi" au "kwa hakika wataita watu wa nyumba yake majina mabaya zaidi"

Ikiwa wamemwita

"kwa watu wamemwita"

Bwana wa nyumba

Yesu anatumia hiii kama msemo kwa ajili yake

Belzabuli

Hili jina linaweza 1) likaelezwa moja kwa moja kama "Belzabuli" au "2) Kutafsiri kama asili yake, kumaanisha "shetani"

wa nyumba yake

Hii ni sitiari kwa maana ya wanafunzi wa Yesu

Matthew 10:26

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwaelekeza wanafunzi wake kuhusu dhiki wanayopaswa kuivumilia wakati watakapoenda kuhubiri.

msiwahofu wao

Hapa "wao" inamaanisha watu wanaowatenda vibaya wafuasi wa Yesu

hakuna jambo ambalo halitafunuliwa, na hakuna lililojifichwa ambalo halitajulikana

Hizi sentensi zote mbili zinamaanisha kitu kilekile. Yesu anasisitiza kuwa Mungu atayafichua mabo yote. Hii inaweza kutafasiriwa katika mafumo tendaji. "Mungu atafunua mambo ambayo watu wanayaficha."

Kile ninachowaambia gizani, mkiseme nuruni, na mnachokisikia kwa ulaini masikioni, mkitangaze mkiwa juu ya nyumba

Sentensi zote hizi mbili zinamanisha kitu kilekile. Yesu anasisitiza kuwa wanafunzi wanapaswa kumwambia kila mmoja kile anachowaambia wanafunzi sirini. "Waambie watu mchana kile ninachokuambia gizani, na tangazeni mkiwa juu ya nyumba kile mnchosikia kwenye masikio yenu"

Kile ninachokuambia gizani

Hapa "giza" linamaanisha "sirini" Ninachowaambia kisirisiri" au "mambo ninayowaambia peke yenu"

kile ninachokisema nuruni

Hapa neno :nuruni" linamaanisha "kwa uwazi. "Semeni kwa uwazi" au "semeni katika umma"

Kile mnachokisikia kwa ulaini masikioni mwenu

Hii ni namna ya kusema kunakomaanisha kunong'ona. "Kile ninachowanong'onezea"

mkitangaze mkiwa juu ya nyumba

mapaa ya nyumba wakati wa Yesu yalikuwa ya bapa, hata watu wali mbali wangeweza kumsikia mtu anapokuwa anaongea kwa sauti ya juu. Hapa mapaa ya nyumba yanamaanisha mahali popote ambapo watu wanaweza kusikia. "Ongea kwa sauti katika eneo la umma ili watu wote wasikie"

Matthew 10:28

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwaelekeza wanafunzi wake juu ya dhiki amabyo wanapaswa kuivumilia wakati watakapoenda kuhubiri

Melezo kwa ujumla

Hapa Yesu pia anaanza kutoa sababa kwa nini wanafunzi wake hawapaswi kuiogopa dhiki ambayo itawapata.

Msiwaogope wale wanaoua mwili lakini hawana uwezo wa kuua roho

Hii haina maana ya kutenganisha kati ya watu wanaoweza kuua mwili na wale wanaoweza kuua roho. Hakuna mtu anayeweza kuua roho. "Msiwaogope watu. Wanaweza kuua mwili, lakini hawawezi kuua roho"

Kuua mwili

Hii inamaanisha kusababisha mauti ya mwili. Ikiwa maneno haya ni magumu, yanaweza kutafsiriwa kama "kukua wewe" au "Kuua watu wengine."

mwili

Sehemu ya mtu inayoweza kuguswa, tofauti na roho au nafsi isiyoweza kuguswa.

kuua roho

kudhuru watu baada ya kufa

roho

sehemu ya mwanadamu ambayo haiwezi kuguswa na ambayo inaishi baada ya kifo cha mwili

mwogopeni yule anayeweza

unaweza kuongeza "kwa sababu" ili kufafanua kwa nini watu wamwogope Mungu. "Mwogopeni Mungu kwa sababu yeye anaweza"

Je, mashomoro wawili hawauzwi kwa senti ndogo

Yesu anaieleza mithali hii kwa njia ya swali kuwafundisha wanafunzi wake. "Fikiria kuhusu mashomoro . Wana thamani ndogo sana kiasi kwamba unaweza kuwanunua wawili kwa salafu kidogo.

Mashomoro

Hawa ni ndege wadogo, wanaokula mbegu. "ndege wadogowadogo"

sarafu ndogo

Hii mara nyingi inatafsiriwa kama sarafu yenye thamani ndogo kabisa katika nchi. inamaanisha sarafu ya shaba thamani yake ni sawa na sehemu ya kumi na sita ya malaipo ya kibarua. "kiasi kidogo cha fedha"

hakuna anayeweza kuanguka chini bila baba yenu kufahamu

Haya maelezo yanaweza kutafsiriwa kataika mfumo tendaji. "Baba yenu anafahamu hata shomoro mmoja akifa na kuanguka chini"

Baba

Hii ni sifa muhimu ya Mungu

Hata idadi ya nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa

Hii inaweza kuelezeka katika mfumo tendaji. "Mungu anajua hata kiasi cha nywele kichwani pako"

zimehesabiwa

"zimehesabiwa"

Mnathamani zaidi kuliko kasuku wengi

"Mungu anawathamini kuliko mashomoro wengi"

Matthew 10:32

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwaelekeza wanafunzi wake kuhusu sababu kuhofia dhiki ambayo itawapata

yeyote atakayenikiri mbele za mtu

"yeyote atakayewaambia wengine huyo ni mwanafunzi wangu" au "Yeyote anayekubali mbele za wengine kwamba yeye ni mwamanifu wangu"

nami pia nitamkiri mbele ya baba yangu aliye mbinguni

Unaweza kuifafanua hiyo ili ieleweke wazi. "nami nitamkiri mbele za Mungu wangu aliye mbinguni kwamba hawa watu ni wangu"

Babab yangu aliye mbinguni

"Baba wa mbinguni"

Baba

Hii ni sifa muhimu ya Mungu"

yeyote atakayenikana mbele za mtu

"yeyote atakayenikana mbele za watu" au "yeye atakayenikataa mbele za watu" au "yeyote atakayekataa kunitambua mimi kwa wengine kuwa yeye ni mwanafunzi wangu"

Nami nitamkana mbele ya Babayangu wa mbinguni

Unaweza kulifafanua kwa uwazi unaoweza kueleweka. "Nitamkana mbele ya Baba aliye mbinguni kuwa huyu ni wangu"

Matthew 10:34

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwaelekeza wanafunzi wake kuhusu sababu kutohofia dhiki ambayo itawapata.

Msifikiri

"Msidhani" au "msilazimike kufikiri"

duniani

Hii inamaanisha watu wanaoishi duniani. "kwa watu wa duniani" au "kwa watu"

upanga

Hii inamaanisha mgawanyiko, mapigano, na mauji kati ya watu

weka

"kugeuka" au "kugawanya" au "kutenganisha"

mtu dhidi ya baba yake

"mwana dhidi ya baba yake"

Adui wa mtu

"Adui wa mtu" au "Adui mbaya wa mtu"

wale wa nyumbani mwake

"watu wa familia yake"

Matthew 10:37

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwaelekeza wanafunzi wake kuhusu sababu kutohofia dhiki itakayowapata.

Yeye ambaye ....hanistahili

Hapa "ana" anamaanisha mtu yeyote kwa ujumla. "Wale ambao ... hawastahili" au "Kama uta... haustahili"

anampenda

Neno la "upendo" hapa linamaanisha upendo wa ndugu" au "upendo kutoka kwa rafiki." "KuMjali" au "aliyejitoa kwa" mwenye kupenda"

anayestahili

"anafaa kuwa wangu" au "anastahili kuwa mwanafunzi wangu"

beba msalaba na kunifuata

"bebea msalaba wake na kunifuata" Huu ni mfano wa kuwa tayari kufa. Kubeba msalalba inamaanisha utayari wa kuteseka na kufa. "lazima anitii kiasi cha kukubali kuteseka na kufa"

beba

"chukua" au "beba na kunyanyua"

Yeye atakayetafuta...atayapoteza...yeye atakayeyapoteza...atayapata

Yesu anatumia mithali kuwafundisha wanafunzi wake. Haya yatafsiriwa kwa maneno machache kwa kadri iwezekanavyo. "Wale wanaotafuta... watayapoteza ... wale wanaoyapoteza ... watayapata" au "wakaoyapata ... uta watakaopoteza ... watapata" au "ikiwa utayapata ... utakosa ... ikiwa utayakosa...utayapata."

atayapata

Hii ni sitiari ya "kutunza" au "kuhifadhi"" jaribu kuhifadhi" au "jaribu kutunza"

atayapoteza

Hii haina maana kwamba mtu atakufa. Ni sitiari " inayomaanisha kuwa mtu hatakuwa na maisha mazuri ya kiroho na Mungu. "Hatakuwa na maisha ya kweli"

anayepoteza maisha yake

Hii haimanishi kufa. Ni sitiari Inayomaanisha mtu kumtii Yesu ni muhimu zaidi kuliko maisha yake. "ambaye anayejikana"

kwa ajili yangu

"kwa sababu ananitumaini mimi" au "kwa ajili yangu" au "kwa sababu yangu" Hili ni wazo lile lile kama "kwa ajili yangu" katika 10:6

yeye ambaye hatabeba ...hana

Tafsiri nyingine:"Wale ambao hawatabeba....sio" au "ikiwa hautabeba...wewe sio" au "endapo utakapobeba ... wewe sio

atayapata

Huu msemo maana yake "atapata maisha ya kweli"

Matthew 10:40

Sentensi unganishi.

Yesu anaendelea kuwaelekeza wanafunzi wake kuhusu kutohofia dhiki itakayowakabili.

Yeye atakaye

Neno "yeye" linamaanisha mtu yeyote. "yeyote" au "yeyote ambaye" au " ambaye"

atakayewakaribisha

Inamaanisha kumkaribisha mtu kama mgeni

Wa

Kiwakilishi "wa" kinamaanisha mitume kumi na wawili ambao Yesu anawaaambia.

ananikaribisha mimi

Yesu anamaanisha ni sawa na kumkaribisha yeye. "ni kama ananikaribisha mimi" au "ni kama vile alikuwa ananikaribisha mimi"

kumkaribisha yeye aliyenituma

Hii inamaanisha wakati mtu anamkaribisha Yesu ni sawa na kumkaribisha Mungu. "ni kama vile kumkaribisha Mungu aliyenituma"

Kwa sababu ni nabii

Hapa kiwakilishi cha "ni" kinamaanisha mtu anayekaribishwa.

thawabu ya nabii

Hii inamaanisha zawadi ambayo Mungu anampa nabii. wala siyo zawadi ambayo nabii anampatia mtu mwingine.

mtu wa haki

Hapa "wa" haimaanishi mtu anayekaribisha. Inamaaanisha mtu anayekaribishwa.

thawabu ya mtu wa haki

Hii inamaanisha zawadi ambayo Mungu humpa mtu wa haki, siyo zawadi ambayo mtu wa haki humpatia mtu mwingine.

Matthew 10:42

Sentensi unganishi

Yesu anamalizia kuwaelekeza wanafunzi wake kuhusu kitu cha kufanya na nini watarajie watakapoenda kuhubiri.

yeyote atakayempatia

"yeyote ambaye atampatia."

mmoja wa wadogo hawa

"mmoja wa hawa wanyenyekevu" au "hawa wasio wa muhimu," Kirai "mmoja wa" mmoja kati ya wanafunzi waYesu.

kweli ninwaambia

"Ninawambia ukweli." Kirai hiki kinongeza msisitizo wa kile Yesu atakachokisema baadaye.

hawezi... kukosa thawabu yake

Kiwakiloishi "ha" na "yake" kinamaanisha mtu yule anayetoa.

yeye hawezi kukosa kwa njia yeyote thawabu yake

"kwamba mtu hakika atapokea thawabu yake"

hawezi kukosa kwa njia yeyote

"Mungu hatamkana." "kukanwa" Hii haimanishi kutoweka kwa mali. Hii inaweza kuelezeka kwa mfumo tendaji. "Kwa hakika Mungu atampatia"

Matthew 11

Mathayo 11 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri huingiza kidogo mistari ya nukuu kutoka kwa Agano la Kale. ULB inafanya hivyo kwa mistari ya nukuu zilizotajwa katika 11:10.

Wasomi wengine wanaamini kwamba Mathayo 11:20 huanzisha hatua mpya katika huduma ya Kristo kwa sababu ya kukataliwa kwake na Israeli.

Dhana maalum katika sura hii

Ufunuo uliofichwa

Baada ya Mathayo 11:20, Yesu anaanza kufunua habari kumhusu yeye mwenyewe na kuhusu mipango ya Mungu Baba, huku akificha habari hii kwa wale wanaomkataa. (Angalia: Mathayo 11:25)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Ufalme wa mbinguni umekaribia"

Maneno haya yana umuhimu mkubwa wa kitheolojia. Wataalam wanajadili ikiwa "ufalme wa mbinguni" ulikuwepo wakati huu au bado unakuja. Tafsiri za Kiingereza mara nyingi hutumia maneno "karibu," lakini hii inaweza kusababisha changamoto katika kutafsiri. Matoleo mengine hutumia maneno "inakaribia" na "yamekaribia."

<< | >>

Matthew 11:1

Maelezo kwa ujumla

Huu ni mwanzo wa sehemu mpya wa simulizi amabapo mwandishi anaonesha jinsi ambavyo Yesu aliwaijibu wanafunzi wa Yohana Mbatizaji.

Ikawa baada ya

Hiki kirai kinaibadilisha kutoka habari ya mafundisho ya Yesu kwenda kile kilichotokea baadaye. "Kisha" au "baadaye"

Kuwaelekeza

"kufundisha" au "kuamurisha".

wanafunzi wake kumi na mbili.

Hii inawahusu wale mitume kumi na wawili waliochaguliwa na Yesu.

katika miji yao

Kimilikishi "yao" kinamaanisha Wayahudi wote kwa ujumla

Sasa

Neno hili limetumika hapa kuonesha mwanzo katika habari kuu. Mathayo anaanza kusimulia habari mpaya

Na Yohana akiwa gerezani aliposikia juu ya

"Wakati Yohana, akiwa gerezani aliposikia juu ya" au "Yohana alipoambiwa na mtu, wakati akiwa gerezani kuhusu, "Ingawa Mathayo hajawaambia wasomaji kwamba mfalme Herode alikuwa amemfunga gerezani Yohana mbatizaji, wasomaji wa kwanza wangekuwa wanaielewa habari na maana yake. Mathayo atatoa habari za Yohana mbatizaji baadaye, kwa hiyo yawezekana si vizuri kufafanua zaidi hapa.

alituma ujumbe kupitia wanafunzi wake.

Yohana Mbatizaji aliwatuma wanafunzi wake ujumbe kumpelekea Yesu.

na wakamuuliza

kiwakilishi "mu'' kinamrejea Yesu.

Wewe ni yule ajaye

"Wewe ndiye yule amabye tunamtarajia kuja." Hii ni namna nyingine ya kumaanisha Masihi au Kristo.

au kuna mwiingine tunayepaswa kumtazamia

''Tunapaswa kumtazamia mwingine." kiwakilishi "tu" kinarejerea ,wayahudi wote, siyo wanafunzi wa Yohana pekee.

Matthew 11:4

mkamtaarifu Yohana

"mwambieni Yohana''

wakoma wanatakaswa

Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo tendaji. "Ninawaponya wenye ukoma"

Watu waliokufa wanafufuliwa

Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji. " Ninawafanya wale waliokufa kuwa hai tena

Watu wahitaji wanahubiriwa habari njema

Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji "Ninawaambia wahitaji"

yule asiyeona shaka juu yangu

Hapa neno "shaka" ni nahau inayomaanisha kupoteza imani. "mtu asiyeachca kuamini kwa sababu ya kile ninachofanya" au "mtu asiyeona mashaka kwa sababu yangu"

Matthew 11:7

Sentensi unganishi

Yesu anaanza kusema na makutano kuhusu Yohana mbatizaji.

Ni nini mlikwenda kuona katika jangwa tete likitikiswa na upepo?

Yesu alitumia swali ili kuwafanya watu wafikiri kuhusu Yohana kuwa ni mtu wa aina gani." Kwa hakika hamkuenda jangwani kuona tete ... upepo.

tete likitikiswa na upepo

Hii inaweza kumaanisha 1) majani halisi ya mto Yorodani au 2) Yesu anatumia sitiari kumaanisha aina ya mtu. "mtu anayebadili fikra zake ni kama tete linalopeperushwa na upepo.

likitikiswa na upepo

Hii inaweza kutafsirwa katika mfumo tendaji. "yumbishwa na upepo" au "peperushwa na upepo"

Lakini ni nini mlikwenda kuona _ mtu aliyevaa mavazi?

Yesu anatumia swali ili kuwafanya watu wafikiri juu ya Yohana kuwa ni mtu wa aina gani. Kwa kweli hamkwenda jangwani ili kuona mtu ... aliyevaa?

aliyevaa mavazi mororo

"kuvaa mavazi yenye gharama kubwa." Watu majiri walivaa mavazi ya aina hii.

Hakika

Hili neno, linaongezea msisitizo kwa kile kinachofuata. "kwa kweli"

nyumba za wafalme

"ikulu za wafalme"

Matthew 11:9

Sentesi unganishi:

Yesu aliendelea kuongea na umati kuhusu Yohana Mbatizaji.

Maelezo kwa ujumla

Katika mstari wa 10, Yesu anamnukuru nabii Malaki kuonyesha kuwa maisha na huduma ya Yohana imetimiza unabii.

Lakini mliondoka kuona nini--nabii?

Yesu anatumia swali ili kuwafikirisha watu juu ya Yohana mbatizaji kuwa ni mtu wa aina gani. "Lakinini kweli kwamba mlienda jajngwani kumuona nabii"

Lakini mlienda nje kuona nini--nabii? Ndiyo, nawaambia nyinyi.

Kiwakilishi cha wingi ''nyinyi'' inarejelea kwa katika hali zote.

ni zaidi ya nabii

Hii inaweza kutafsirika kama sentensi timilifu. "Siyo nabii wa kawaida" au ''siyo mtu wa kawaida'' au ''ni wa muhimu kuliko nabii wa kawaida''

huyu ndiye aliye andikiwa

Hii inaweza kutafsirika katik mfumo tendaji. "Hiki ndicho nabii Malaki aliandika zamamni za kale kuhusu Yohana mbatizaji"

namtuma mjumbe wangu

Kiwakilishi ''na'' na ''wangu'' kinamrejea Mungu. Malaki ananukuu ambacho Mungu alisema.

mbele ya uso wako

Kiwakilishi "wako" ni cha umoja kwa sababu Mungu alikuwa anasema juu ya Masihi katika nukuu.vPia "uso" inamaanisha nafsi timilifu, "mbele yako" au "kutangulia"

ataandaa njia yako

Hii ni sitiari inayomaanisha kuwa mjumbe atawaandaa watu kupokea ujumbe wa Masihi.

Matthew 11:11

Sentensi Unganishi:

Yesu aliendelea kuwaambia makutano juu ya Yohana Mbatizaji

Mimi nawaambia ukweli

"Nawaambia ukweli." Kirai hiki kinaongeza msisitizo wa kile Yesu alichosema baadaye.

kati ya waliozaliwa na wanwake

Hii ni namna ya inayomaanisha watu wote. "kati ya watu wote waliopata kuishi"

Hakuna aliye mkuu kuliko Yohana mbatizaji

Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji. ''Yohana Mbatizaji ni mkuu zaidi" au " Yohana mbatizaji ni wa muhimu zaidi".

aliyemdogo katika ufalme wa mbinguni

Ha " ufalme wa mbinguni" unamaanisha utawala wa Mungu kama mfalme. Kirai "ufalme wa mbinguni" kimetumika katika injili ya Mathayo tu. Kama inawezekana jaribu kutumia "mbinguni" unapotafsiri. "aliye mdogo kabisa katika utawala wa Mungu wetu mbinguni"

ni mkuu kuliko yeye

'' wa muhimu kuliko Yohana''

Tokea siku za Yohana Mbatizajihadi leo

''Tokea muda ambao Yohana alianza kuhubiri ujumbe''

ufalme wa mbinguni ni wa nguvu, na wenye nguvu huuchukua kwa nguvu

Kuna maana nyingi zinzazoweza kumaanisha katika mstari huu. 1) Watu wengine huutumia ufalme wa Mungu kwa malengo yao binafsi. na kwamba wako tayari kutumia nguvu dhidi ya watu wengine ili kutimiza hitaji hili. 2)Tafsiri zingine zingine zinatumia maana sahihi kwamba wito wa kuingia katika ufalme wa mbinguni kimekuwa ni kitu cha muhimu, kwamba watu lazima wapokee kwa kuzingatia kabisa. ili kuupokea wito na kuzuia majaribu ya kufanya uovu. 3 )Watu wenye nguvu wanawadhuru watu wa Mungu na kujaribu kumzuia Mungu asitawale.

Matthew 11:13

Sentensi unganishi

Yesu aliendelea kuongea na umati juu ya Yohana Mbatizaji.

kwa kuwa manabii na sheria, imekuwa ikitabiri mpka kwa Yohana

Hapa neno " manabii na sheria"linamaanisha kile ambacho manabii na Musa waliandika katika maandiko. "Kwa kuwa haya ndiyo mambo ambayo manabii na Musa walitabiri katika maandiko mpaka wakati wa Yohana mbatizaji

na kama mko

Kiwakilishi ''mko''kinarejelea watu katika umati.

huyu ni Eliya, yule ajaye

''Hii inarejelea kwa Yohana Mbatizaji. Hii haimaanishi Yohana Mbatizaji ni sawa na Eliya. Yesu anamaanisha Yohana mbatizaji anatimiza unabii juu ya "Eliya ajaye" au "Eliya anayefuata". "Wakati nabii Malaki aliposema kuwa Eliya atarudi, alikuwa akiongea juu ya Yohana mbatizaji"

Aliye na masiko ya kusikia

Hii ni namna ya kumwambia kila anayesikilza. ''Kila anayenisikiliza''

na asike

Hapa ''asikie" inamaanisha kuwa msikivu. " lazima awe mwangalifu kwa kile nisemacho''

Matthew 11:16

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuongea na makutano juu ya Yohana Mbatizaji.

Nikilinganishe na nini

Yesu anaitumia swali kutoa mlinganisho kati ya watu wa nyakati zile na kile amabacho watoto wanaweza kusema katika eneo la soko. "Hivi ndivyo kizazi hiki kilivyo"

kizazi hiki

''watu wanaoishi sasa'' au ''watu hawa'' au ''ninyi watu wa kizazi hiki''

Ni mfano wa watoto wanaocheza maeneo ya sokoni ... na hamkulia

Yesu anatumia mfano kuwaelezea watu waliokuwa hai kipindi hicho. Anawalinganisha na kikundi cha watoto wanaojaribu kuwavuta watoto wengine ili wacheze nao. Lakini haijarishi aina ya mbinu yeyote wanayotumia, wale watoto wengine hawataungana nao. Yesu anamaanisha kuwa haijalishi kama Mungu alimtuma mtu kama Yohana mbatizaji, anaishi nyikani na kufunga, au mtu kama Yesu, ambaye anasherehekea na wenye dhambi bila kufunga. Watu, hususani Mafarisayo na viongozi wa dini, bado wanabaki wasumbufu na wanakataa kuupokea ukweli wa Mungu

maeneo ya soko

eneo kubwa, la wazi ambapo watu walikuja kuuza na kununu bidhaa zao.

tuliwapigia zomari

''tu'' inarejelea watoto waliokuwa wamekaa katika maeneo ya soko. ''wa'' ni wingi na inarejelea lile kundi lingine la watoto

na hamukucheza

''lakini hamukucheza ule muziki mzuri''

tuliomboleza

Hii inamaanisha waliimba nyimbo za huzuni kama vile wanawake wafanyavyo kwenye mazishi.

na hamukulia

''lakini hamukulia pamoja nasi''

Matthew 11:18

Sentensi unganishi:

Yesu anahitimisha kuongea na makutano kuhusu Yohana Mbatizaji.

bila kula mkate au kunywa mvinyo

Hapa "mkate" unamaanisha chakula. Haimanishi kuwa Yohana alikuwa hali chakula. Inamaanisha kuwa alikuwa anafunga mara kwa mara na alipofungua hakula vizuri, chakula cha gharama. "Mfungo endelevu na kutokunywa pombe" au "kutokula chakula kizuri na kutokunywa divai"

walisema, 'ana pepo.'

Hii inaweza kutafsiriwa kama nukuu ya mojakwa moja. ''wanasema kwamba ana pepo'' au ''walimtuhumu kuwa na pepo.''

wanasema

Matukio yote ya "wali" yanamaanisha watu wa kizazi kile, na zaidi sana mafarisayo na viongozi wa dini.

Mwana wa Adamu

Yesu anamaanisha yeye mwenyewe. " Mimi mwana wa Adamu"

alikuja akila nakunywa

Hiki ni kinyume cha tabia ya Yohana. Hii ni zaidi ya kula kiasi cha kawaida cha chakula na kinywaji. Inamaanisha Yesu alisherehekea na kufurahia chakula na kinywaji kizuri kama vile watu wengine walivyofanya.

wakasema, anagalia, ni mtu mlaji

Hii inaweza kutafsiriwa kama nukuu ya moja kwa moja. "wanasema kuwa ni mlaji" "wanamtuhumu kuwa anakula sana" Kama ulitafasiri "Mwana wa mtu" kama "Mimi, Mwana wa mtu," Ile nukuu ya moja kwa moja inaweza kutafsiriwa kama "wanasema kwamba mimi ni mlaji"

mlevi

"mlevi" au "hunywa pombe nyingi daima."

Lakini hekima huthibitishwa kwa mataendo yake

Hii ni mithali ambayo Yesu anaitumia katika mazingira haya, kwa sababu watu waliomkataa yeye na Yohana walikuwa hawapati hekima. Yesu na Yohana mbatizaji ni watu wa hekima, na ,matokeo ya matendo yao yanathibitisha.

Hekima huthibitiswa kwa matendo yake

Hapa "hekima" imefafanuliwa kama mwanamke aliyethibitishwa kuwa ni mwema kwa matendo yake. Yesu anamaanisha kuwa matokeo ya matendo ya mtu huthibitisha kuwa ni mwenye hekima. "Hii inawza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Matokeo ya matendo ya mtu humthibitisha kuwa ni mwenye hekima"

hekima inaonekana

Haya maelezo, Yesu anafafanua hekima kama vile ilikuwa ni mwanamke, haitumiki hapa kwa namna kwamba hekima inatoa haki mbele ya Mungu ila kwamba hekima inaonekana haki.

Matthew 11:20

Maelezo kwa ujumla:

Yesu alianza kuwakemea watu wa miji ambayo alianza kufanya miujiza.

kukemea miji

Hapa "miji" inamaanisha watu walioishi kwenye hiyo miji. "alikemea watu wa miji hiyo"

miji

''miji''

ambamo baadhi ya matendo yake makuu yalitendekea

Hii inaweza kutafsiriwa kwa mfumo tendaji ''ambamo baadhi ya matendo yake makuu yalitendekea''

Matendo makuu

" matendo makubwa" au " kazi za nguvu ya Mungu" au "miujiza"

Ole kwako, Kolazini! Ole kwako, Bethsaiida!

Yesu anaongea kiasi kwamba watu wa miji ya Kolazini na Bethsaida walikuwa pale wakimsikiliza, lakini hawakuwa wao.

kwa sababu hawakutubu

Kiwakilishi ''hawa'' inarejelea kwa watu wa miji ile ambayo haikutubu.

Kama matendo makuu yangetendeka ... kwa kuvaa magunia na kujipaka majivu

Yesu anafafanua kwa kubuni kuwa kama yangekuwa yametokea huko nyuma, lakini haikotokea

Kama matendo makuu yangetokea Tiro na Sidoni yale yaliyotendeka kwako

Hii inaweza kutafsiriwa kwa mfumo tendaji. "Kama ningefanya matendo makubwa katika watu wa Tiro na Sidoni ambayo nimeyafanya kwenu"

Yale yaliyotendeka kwako ... kwako

Kiwakilishi cha "kwako" ni cha wingi na kinamaanisha Korazini na Bethisaida. Kama tafsiri hii si kawaida ya lugha yako, utumie neno lenye maana mbili likimaanisha miji miwili au kiwakilishi cha wingi cha "ninyi" kwa kumaanisha watu wa miji ile.

Wangekuwa wametubu zamani

Kiwakilishi "wa"kinarejelea watu wa Tiro na Sidoni.

wangetubu

"inaonesha walihuzunishwa na dhambi zao"

Itakuwa uvumilivu kwa Tiro na Sidonisiku ya hukumu kuliko kwako

Hapa " Tiro na Sidoni'' zinamaanisha watu wanoishi kwenye hiyo miji. "Mungu ataonyesha huruma zaidi kwa watu wa Tiro na Sidoni katika siku ya hukumu kuliko ninyi" au "Mungu atawapa adhabu kalizadi katika siku ya hukumu kuliko watu wa Tiro na Sidoni"

kuliko kwako

maelezo kusudiwa yangewekwa wazi. "kuliko kwako, kwas sabasbu haukutubu na kuniamini, ingawa ulioniona nikifanya miujiza"

Matthew 11:23

Sentensi unganishi:

Yesu anaendelea kukemea miji ambayo miujiza yake ilitendeka karibuni.

Wewe, Kapernaum

Yesu sasa anaongea na watu wa mji wa Kapernaum kama vile walikuwa wanamsikiliza, lakini walikuwa hawasikilizi. Kiwakilishi ''wewe'' ni cha umoja kinarejelea Kapernaum kwa mistari yote miwili.

wewe

Matukio yote ya kiwakilishi cha "wewe" yakao katika umoja. Kama kinatumika kila mahali kuonyesha watu wa mji, basi kiwakilishi cha wewe kitafsiriwe katika wingi wake

Kapernaum...Sodoma

Majina ya miji hii yametumika kumaanisha watu waliokuwa wanaishi Kapernaum na Sodoma.

unadhani utainuliwa hadi mbinguni?

"unadhani utainuliwa hadi mbinguni ?" Yesu anatumia balagha kuwakemea watu wa Kapernaum kwa majivuno yao. "inaweza pia kutumika kwa mfumo tendaji. "huwezi kujiinua mwenyewe hadi mbinguni" au "sifa za watu wengine haziwezi kukuinua hadi mbinguni kama unavyodhani atafanya"

utashuswa hadi chini kuzimu

Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji ''Mungu atakupeleka hadi kuzimu.''

Kama katika Sodoma ... ingekuwepe hadi leo

Yesu anatumia mazingira ya kubuni ambayo yangetokea katika siku zilizopita, lakini haikutokea.

matendo makuu

''''matendo makuu'' au ''kazi ya nguvu za Mungu'' au "miujiza"

ingekuwepo hadi leo

Kiwakilishi ''inge'' kinarejelea kwa mji wa Sodoma

nasema kwako

Kirai hiki kinaongeza msisitizo wa kile Yesu alichosema baadaye

itakuwa rahisi kwa nchi ya Sodoa kusimama katika siku ya hukumu kuliko wewe

Hapa "nchi ya Sodoma" inamaansha watu walioishi kule. ''Mungu ataonyesha rehema kwa watu wa Sodoma katika siku ya hukumu kuliko kwako'' au Mungu atawapa adhabu kali zaidi katika siku ya hukumu kuliko watu wa Sodoma.''

kuliko wewe

Taarifa zilizofumbwa ziwekwe wazi. "kwa sababu haukutubu na kuniamini, ingawa uliniona nikifanya miujiza"

Matthew 11:25

Maelezo kwa ujumla:

katika mstari wa 25 na 26, Yesu anomba kwa baba yake aliye mbinguni wakati akiwa bado katika uwepo wa makutano. Katika mstari wa 27, anaanza kusema na watu tena.

Baba

Hi ni sifa muhimu ya Mungu

Bwana wa mbingu na nchi

"Bwana anayetawala mbingu na nchi" Kirai cha mbingu na nchi ni cha mlinganyo wa jumla amabcho kinaonesha watu wote na vitu vyote duniani. ''Bwana atawalaye ulimwenguni kote"

uliwaficha mambo haya ... na kuyafunua

Haiko wazi ina maanisha nini kwa ''mambo haya.'' Kama lugha yako inahitaji kuweka maana halisi, tafsiri nzuri ni hii ''umeuficha ukweli huu na kuwafunulia"

umewaficha mambo haya

''umewaficha mambo haya '' au ''haujafanya mambo haya kueleweka kwao.'' Hili tendo ni kinyume cha ''kufunuliwa.''

wenye hekima na ufahamu

Hizi nomino sifa zinzweza kutafasiriwa kama visifa ''kutokawatu wenye hekima na ufahamu.''

na kuyafunua

"kuyafanya yafahamike." kiwakilisha "ya" kinamaanisha "mambo haya" viko mwanzoni katika mstari huu.

kwa wasio na elimu,

"kwa wajinga"

kama watoto wadogo

Yesu anamlinganisha mtu asiye na elimu na mtoto mdogo. Yesu anasisitiza kwamba wengi wa wale wanaomwamini ni watu wasio na elimu au wanaojidhania kuwa si wenye elimu

kwa kuwa ilikupendeza hivyo machoni pako

kupendeza machoni pako - Hi kirai "machoni pako" ni sentensi mbadala ionyeshayo jinsi mtu apendavyo kitu kuwa ni cha muhimu. "kwa vile ilikupendeza kuwa ni vizuri kufanya hivi"

Mambo yote yamekabidhiwa kwangu kutoka kwa baba yangu

Hii inaweza kutafasiriwa kwa muundo tendaji: ''Baba yangu amekabidhi mambo yote kwangu'' au ''Baba yangu ameweka kila kitu kwangu."

Mambo yote

Maana kusudiwa ni 1)Mungu Baba amefunua kila kitu kuhusu yeye na ufalme wake kwa Yesu. aua 2) Mungu ametoa mamlaka yote kwa Yesu

Baba yangu

Hii ni sifa muhimu ya Mungu amabyo inaonyesha uhusiano kati ya Yesu na Mongu

hakuna amjuaye Mwana isipokuwa Baba

''Ni Baba pekee amjuaye Mwana.''

hakuna ajuaye

Nyakati zote Yesu hutumia kirai hiki, neno "ajuaye" linamaanisha zaidi ya kumjua mtu. Linamaanisha kumjua mtu kwa undani kwa sababu wanauhusiano maalumu

Mwana pekee

Yesu alikuwa anajirejelea yeye mwenyewe binafsi katika nafsi ya tatu.

mwana

Hii ni sifa ya muhimu ya Yesu mwana wa Mungu

hakuna amjuaye Mwana isipokuwa Baba

''Ni Mwana pekee amjuye Baba''

hakuna amjuaye Baba isipokuwa mwana pekee

"ni mwana pekeeamjuaye Baba

na yeyote ambaye Mwana ana hamu kumfunulia

"na watu wale ambao mwana anapenda kuwafunulia jinsi Mungu alivyo"

Matthew 11:28

Sentensi unganishi

Yesu anamalizia kuongea na makutano.

ninyi nyote

Viwakilishi vyote vya "niniyi" ni vya wingi

mnaolemewa na mzigo mizito

Yesu anaongea kwa watu kama na wanyama, amabao bwana zao wamewabebesha mizigo migongoni mwao. Hii ni sitiari kwa ajili ya Sheria na kanuni ambaazo viongozi wa Kiyahudi waliwabebesha watu ili kuzitii. "msumbukao na sheria ambazo mmebeshwa na viongozi wa dini"

Nitawapumzisha

''Nitawaruhusu nyinyi kupumzika kazi na mizigo''

Mimi ni mnyenyekevu na mpole wa moyo

Hapa neno"mpole" na "mnyenyekevu wa moyo" ki msingi yanamaanisha kitu kilekile. Yesu anayaunganisha kuongeza msisitizo kuwa atawajali kwa upole zaidi kuliko vioingozi wa . dini. "mimi ni mpole na mnyenyekevu" au "mimi ni mpole sana"

Jitieni nira yangu

Yesu anaendelea kutumia sitiari. Yesu anawakaribisha watu kuwa wanafunziwake na kumfuata"

mtapata pumziko la nafsi zenu

Hapa "nafsi" inamaanisha mtu kamili. "mtapumzikia ninyi wenyewe" au "mtaweza kupumzika"

kwa kuwa nira yangu ni laini na mzigo wangu ni mwepesi

Virai vyote hivi vinamaanisha kitu kilekile. Yesu anasisitiza kuwa ni rahisi kumtii yeye kuliko sheria za Wayahudi. "kile nitakacho wabebesha kitakuwa ni chepesi"

Mzigo wangu ni mwepesi

Neno "mwepesi" hapa ni kinyume cha kizito, siyo kinyume cha giza.

Matthew 12

Mathayo12 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri hupendelea huingiza kidogo mistari ya nukuu za Agano la Kale. ULB na tafsiri nyingine nyingi za Kiingereza huingiza mistari yote ya 12: 18-21, ambayo ni nukuu kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

Sabato

Kutii Sabato ni sehemu muhimu katika sura hii. Hata hivyo, Yesu anafafanua kati ya kufuata Sabato jinsi Mungu alivyoamuru na kufuata sheria ambazo Mafarisayo waliziunda kuhusu Sabato. (Angalia: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sabbath)

"Kukufuru Roho"

Kuna utata mkubwa juu ya kutambua vizuri dhambi hii maalum. Hata hivyo, inaonekana kuwa inahusisha kumtukana Roho Mtakatifu na kazi yake. Kwa kuwa sehemu ya kazi yake ni kuwashawishi watu kuwa wao ni wenye dhambi na kwamba wanahitaji msamaha wa Mungu, yeyote ambaye alikejeli ukweli huu hangetaka kuja kwake Mungu kwa toba. Kwa sababu hii, hangeweza kusamehewa. (Angalia: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Kaka na Dada

Sura hii inaanzisha dhana ya kaka na dada "wa kiroho". Maandiko hutumia maneno haya kwa kutaja uhusiano kati ya Waisraeli. Hapa, wale wanaomfuata Yesu sasa wanajulikana kama kaka na dada. (Angalia: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#spirit na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#brother)

<< | >>

Matthew 12:1

Maelezo kwa ujumla:

Huu ni mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi ambapo mwandishi anazungumza juu ya kukua kwa upinzani kwa huduma ya Yesu. Hapa, Mafarisaya wanawakosoa wanafunzi wa Yesu kwa kuvuna nafaka ya ngano siku ya sabato.

Wakati huo

Hii inaonyesha mwanzo mpya wa simulizi. "Baadaye kidogo"

shamba la nafaka

sehemu ya kupanda nafaka. Kama ngano haifahamiki na "nafaka" ni neno la jumla sana, basi waweza kutumia "shamba" la mazao ambayo wanatengeneza mikate."

kuvunja masuke ya nafaka na kuyala...wanajunja sheria ya sabato

Kuvuna nafaka kwenye mashamba ya wengine na kula haikuchukuliwa kuwa ni kuiba. Swali lilikuwa kama mwingine angeweza kufanya shughuli hii kisheria katika siku ya sabato.

kuyavunja masuke na kuyala

"kuchukua baadhi ya ngano na kula" au "kuchukua baadhiya mbegu za ngano na kula"

masuke ya nafaka

Hii ni shsemu ya juu ya mmea wa ngano ambayo ni aina ya jani kubwa. Hushikilia nafaka iliyokomaa au mbegu za mmea.

Mafarisayo

Hiihaimanisha mafarisayo wote. "baadhi tu ya mafarisayo"

Tazama

"angalia." Mafarisayo hutumia neno hili kupata usikifu wa kile wanafunzi wa Yesu walichokuwa wakifanya.

Matthew 12:3

Sentensi unganishi

Yesu anajibu ukosoaji wa mafarisayo

akawaambia

Mafarisayo

Hamjasoma ... nao

Yesu anatumia swali kujibu ukosoaji wa mafarisayo. Yesu anawapa changamoto ili kufikiri juu ya maana ya andiko ambalo walisoma. "Najua mmesoma juu yaa...nao"

nyumba ya Mungu

Wakati wa Daudi bado hapakuwa na hekalu. "hema" au " mahali pa kumwabudia Mungu"

mkate wa wonyesho

Huu ni mkate uliotakaswa ambao makuhani walipeleka mbele za Mungu hemani. "Mikate ambayo makuhani walipeleka mbele za Mungu

wale aliokuwa pamoja nao

"watu waliokuwa pamoja na Daudi"

ila halali kwa makuhani

"ni makuhani tu walioruhusiwa kuula."

Matthew 12:5

Sentensi unganishi:

Yesu anaendelea kuwaitikia Mafarisayo.

bado hamjasoma katika sheria ... lakini hawana hatia

Yesu antumia swali kijbu hoja za mafarisayo. Yesu anawataka wafikirie maana yakile walichosoma katika maandiko. "And, na mmesoma katika sheria za Musa... lakini hawana hatia.

huinajisi Sabato

"kufanya katika sabato ambayo wangefanya katika siku nyingine."

hawana hatia

" Mungu hatawaadhibu" au "Mungu hatawaonea hatia"

nasema kwenu

Hiki kinaongeza msisitizo kwa kile alichosema baadaye.

aliye mkuu kuliko hekalu

" aliye wa muhimu zaidi kuliko hekalu." Yesu alikuwa anarejelea kwake yeye mwenyewe kama mmoja aliye mkuu.

Matthew 12:7

Sentensi unganishi:

Yesu anaendelea kuwajibu Mafarisayo

Maelezo kwa ujumla:

Katika mstari 7, Yesu anamnukuu nabii Hosea kuwakemea Mafarisayo.

Kama mngalijua hii inamaanisha nini, nataka rehema na siyo dhabihu; msingaliwahukumu wasio na hatia

Hapa Yesu ananukuu andiko. "Nabii Hosea aliandika juu ya haya tangu zamani. "Natakarehema na siyo dhabihu. 'Kama mngalielewa hii ilimaanisha nini, msingaliwalaumu wasio na hatia'

Nataka rehema na sio dhabihu

Katika sheria za Musa, Mungu aliwaagiza Waisraeli kutoa sadaka. Hii inamaanisha kuwa Mungu huichukulia rehema kuwa muhimu kuliko sadaka.

hii inamaanisha nini

"nini Mungu amesema katika maandiko"

Nataka

Kiwakilishi "Na" kinamrejelea Mungu.

wasio na hatia

Hii inaweza kutafsiriwa katika muundo tendaji. "Wale wasiokuwa na hatia"

Mwana wa Adamu

Yesu anamaanisha yeye mwenyewe

ndiye Bwana wa Sabato

"anaitawala Sabato" au "anatengeneza sheria juu ya nini watu wanaweza kufanya siku ya Sabato"

Matthew 12:9

Maelezo kwa ujumla

Hapa mandhari yanahamia kwenye kitu kingine mahali ambapo mafarisayo wanamkosoa Yesu kwa kumponya mtu siku ya Sabato.

Kisha Yesu akaondoka pale

"Yesu akaondoka kwenye lile shamba la ngano" au "Kisha Yesu akaondoka"

Sinagogi lao

"singogi" Hapa "lao" inamaanisha Wayahudi kwa ujumla na wala si Mafarisayo tu, kutokana na kipengere kilichopita.

Tazama

Neno " tazama" linatuelekeza kwa mtu mwingine katka simulizi. Lugha yako inaweza kuwa na njia ya kulifanya hili.

mtu aliyepooza mkon

"mtu alikuwa namkono uliopooza" au "mtu mwenye ulemavu wa mkono"

Mafarisayo wakamuuliza Yesu wakisema . J"e, ni halali kumponya mtu siku ya Sabato? Ili kwamba waweze kumshitaki kwa kutenda dhambi

"Mafarisayo walitaka kumshitaki Yesu kwa kutenda dhambi, kwa hiyo walimuuliza, 'Je, ni halali kuponya siku ya Sabato?"

Je, ni halali kuponya siku yaSabato?

Kwa mjibu wa sharia za Musa, Yawezekana mtu kumponya mtu mwingine siku ya Sabato?"

ili waweze kumshitaki kwa kutenda dhambi

Si tu walitaka kumshitaki Yesu mbele za watu, Mafarisayo walitaka Yesu atoa jibu linalopingana na sheria ili waweze kumpeleka kwa hakimu iwamshitaki kwa kuvunja sheria.

Matthew 12:11

Sentensi ungsnishi

Yesu anjibu hoja za Mafarisayo

Nani kati yenu, ambaye ikiwa ana kondoo mmoja ... hatamshika na kumtoa kwa nguvu ndani ya shimo?

Yesu antumia swali kuwajibu Mafarisayo. Anawapa changamoto ya kufikiri juu ya aina gani ya kazi wanayoweza kuifanya siku ya sabato. "Kila mmoja wenu, kama una kondoo mmoja ... angemshika na kumtoa kwa nguvu

Je, ni kipi chenye thamani, zaidi kwani, si zaidi ya kondoo?

Kirai "kipi chenye thamani zaidi" kinaongeza msisitizo kwenye sentensi. " ni wazi mtu ni wa thamani zaidi ya kondoo!" au "Jaribu kufiri vile mtu alivyo wa muhimu kuliko kondoo"

ni halali kutenda mema siku ya Sabato

"Wale wanofanya mema siku ya Sabato wantii sheria"

Matthew 12:13

Kisha Yesu akamwambia yule mtu nyosha mkono wako

Hii inaweza kutafsiriwa kama nukuu isiyo ya moja kwa moja, "Kisha Yesu akamwamuru yule mtu kunyosha mkono wake"

yule mtu

"yule mtu mwenye mkono uliopoza au " yule mtu mwenye ulemavu wa mkono"

Nyosha mkono wako

"Utoe mkono wako" au "utanue mkon wako"

Akaunyosha

"Yule mtu akaunyosha"

ukapata afyfa

Hii inaweza kutafsiriwa katika muundo tendaji. "ule mkono ukawa na afya tena" au "ukawa salama tena"

kupanga kinyume chake

"wakapanga kinyume chake"

Matthew 12:15

Maelezo kwa ujumla

Simulizi hii inaeleza jinsi matendo ya Yesu yalivyotimiza moja kati ya unabii wa Isaya

Yesu alivyoelewa hili

"Yesu alikuwa anatambua kile Mafarisayo walichokuwa wakipanga

aliondoka hapo

"alitoka" au "aliondoka"

wasije wakamfanya afahamike kwa wengine

wasimwambie mtu yeyote kuhusu yeye"

kwamba itimie ile kweli

Hii inaweza kutafsriwa kama sentensi mpya. "Hii ilitimiza kile"

iliyokuwa imesemwa na nabii Isaya

Hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji. "Kile Mungu alichokuwa amesema zamani kupitia Isaya akaisema..

Matthew 12:18

Sentensi unganishi

Hapa Mthayo anamnukuu nabii Isaya kuonesha kuwa huduma ya Yesu ilitimiza unabii

Tazama

"Angalia." Mungu alitumia neno hili kumleta mtu mwingine

mpe ...Nita

Viwakilishi vyote vinamrejelea Mungu. Isaya ananukuu kile ambacho Mungu alimwambia

katika yeye nafsi yangu imependezwa

Hapa "nafsi" inamanisha nafasi kamil. "na nimependezwa naye"

na atatangaza

"na mtumishi wangu atatangaza"

atatangaza hukumu

Hapa "hukumu" haimaanishi "adhabu" inamaanisha mtumishi atawambia mtaifa Mungu ni mwenye haki, na atawaokoa

Matthew 12:19

Sentensi unganishi

Mathayo anaendelea kumnukuu Isaya

wala awaye yote kusikia sauti yake mitaani

hapa "sauti" inamaanisha nafsi kamili "na hataongea kwa sauti"

yake ... hata

Viwakilishivyote hivi vinamaanisha mtumishi wa Mungualiyechaguliwa

mitaani

Hii ni nahau inayomaanisha "umma."katika miji"

hatalivunja tet liliochubuliwa .. hatazima utambi wowote unatoa moshi

Senttensi hizi zote zinamaanisha kitu kilekile. Ni sitiari zinazosisitiza kuwa mtumishi wa Mungu atakuwa mnyenyekevu na mpole. Vyote "tete lililochubuliwa na utambi utoa moshi" vinawakilisha watu dhaifu na wenye kudhuru.

hatalivunja

"hataliweka nje"

utambi utoa moto

Hii inamaanisha utambi ambao moto umezima lakini bado unatoa moshi

moshi, mpaka

Hii inaweza kutafsiriwa kwa sentensi mpya; "moshi Hiki ndicho atachofanya"

Mpaka atakapoleta hukumu ikashinda

"mpaka atakapofaulu kuleta haki na wokovu kwa watu. Maana ya nomino dhania "hukumu" inaweza kutafsiriwa kama "haki" au "okoa". "watuwajue kuwa mimi ni wa haki na nitawaokoa"

katika jina lake

Hapa "jina" linamaanisha nafsi kamili

Matthew 12:22

Maelezo kwa ujumla

Hapa mandhari yanabadilika na kuongelea wakati mwingine wakati Mafarisyao walipomshitaki Yesu kwa kumponyamtu kwa nguvu za shetani.

Mtu fulani kipofu na bubu, aliyepagawa na pepo aliletwa mbele za Yesu

Hiiinaweza kutafsiriwa katikamfumo tendaji. "Mtu mmoja alimleta kwa Yesu mtu aliyekuwa kipofu na bubu kwa sababu pepo lilikuwa likimtawala"

Mtu kipofu na bubu

"mtu asiyeweza kuona na hawezi kuongea"

Makutano wote walishsangaa

"Watu wote waliomwona Yesu akimponya yule mtu walishangaa"

Mwana wa Daudi

Hi ni sifa ya Masihi au Kristo

Mwana wa

Hapa hii inamaanisha "kizazi cha"

Matthew 12:24

Maelezo kwa ujumla

Katika mastari wa 25, Yesu anaanza kuwajibu mashataka ya Mafarisayo kwamba amemponya mtu kwa nguvu za shatani

muujiza huu

Hii inamaanisha muujiza wa kumponya yule kipofu, bubu na alaiyepagawa na pepo.

Huyu mtu hatoi pepo kwa nguvu zake isipokuwa isipokuwa nguvu za Belzebuli,

Hii inaweza kuelezwa katika muundo chanya. "Huyu mtu anaweza kufukuza pepo kwa sababu ni mtumishi wa Belzabul"

Huyu mtu

Mafarisayo waliepuka kumwita Yesu kwa jina ili kuonesha kuwa hawamkubali.

mkuu wa pepo

"mfalme wa pepo"

kila ufalme uliogawanyika wenyewe huharibika, na kila mji au nyumba iliyogawanyika haitasimama

Yesu anatumia mithali kuwajibu Mafarisayo. Sentenzi hizi mbili zinmaanishakitu kilekile. Zinasisitiza kuwa haimanishi chochote kwa Belzabul kutumia nguvu zake kuwapinga pepo wengine.

Kila ufalme uliogawanyika huharibika

Hpa "ufalme" unamaanisha wale wanaoishi kwenye huo ufalme. Hii inaweza kutafsiriwa katika mfumo tendaji. "Ufalme hautadumu wakati wake wanapigana wao kwa wao"

kila mji au nyumba iliyogawanyika haitasimama

Hapa"mji" unamaanisha watu wanaoishi humo na. "nyumba" inamaanisha familia. "inaharibu mji au familia watu wanapopigana wao kwa wao

Matthew 12:26

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kujibu hoja za mafarisayo za kwamba alimponya mtu kwa nguvu za shetani

ikiwa shetani atamwondoa shetani mwenzake

Matumizi ya pili ya shetani yanamaanisha pepo wanaomtumikia shetani. "Kama shetani atafanya kazi kinyume na pepo zake"

Shetani ... Beelzabul

Majina yote yanamaanisha nafsi moja

ufalme wake utasimama?

Yesu anatumia swali kwapa changamoto Mafarisayo. "Ufalme wa shetani hauwezi kusimama" au "ufalme wa shatani hautadumu"

wafuasi wenu huwatoa kwa njia ya nani

Yesu anatumia swali lingine kuwapa changamoto Mfarisayo. "kisha lazima useme wafuasi wenu pia huwatoa pepo kwa nguvu za beelzabul. Lakini mnajua kuwa hii siyo kweli"

kwa ajili hii watakuwa mahakimu wenu

"Kwa sababu wafuasi wenu huwatoa pepo kwa nguvu za Mungu, wanahakikisha kuwa mmekosea."

Matthew 12:28

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwajibu Mafarisayo

Na kama natoa

Hapa "kama" haimaanishi kuwa Yesuanahoji jinsi anavyowatoa pepo. Hapa Yesu anatumia neno kuleta sentensi ya kweli. "Lakimi kwa sababu nina"

basu ufalme wa Mungu umekuja kwenu

"Basi ufalme wa mbinguni umefika kwenu." Hapa "ufalme" utawala wa Mungu kama mfalme. "Hii inamaanisha Mungu anaanzisha ufame kwenu"

umekuja kwenu

Hapa "kwenu" ni wingi na inamaanisha watu wa Israel,

na mtu awezaje kuingia ndani ya nyumba ... atakapoiba mali yake

Yesu anatumia mfanokuendelea na majibu yake kwa Mafarisayo. Yesu anamaanisha anaweza kuwatoa pepo kwa sababu ana nguvu kuliko shetani.

Awezaje mtu kuingi ... asipomfunga mwenye nguvu kwanza?

Yesu anatuumia swali kuwafundisha Mafarisauo na makutano. "Hakuna awezaye kuingia ..bila kumfunga mwenye nguvu kwanza"

Ndipo atakapoiba

"Ndipo atakapoiba" au "Ndipo atakapoweza kuiba"

yeyote asiyekuwa pamoja nami

"ambaye hashirikiani nami" au "amabye hafanyi kazi p amoja nami"

yuko kinyume changu

"ananipinga mimi" au "hufanya kazi kinyume na mimi"

Huyo asiyekusanya nami hutapanya

Yesu anatumia kirai amabcho kinamunesha mtu amabye aidha anakusanya kundi la wanyama kwa mchungaji au anayewatapanya totka kwa mchungaji.

Matthew 12:31

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwajibu Mafarisayo

nasema kwenu

Hii inaongeza msisitizo wakile Yesu alichosema baadaye

sema kwenu

Hapa "kwenj" ni wingi. Yesu anaongea moja kwa moja na Mafarisayo, lakini pia anwafundisha makutano

kila dhambi na kufuruwatu watasamehewa

Hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji. "Mungu atasamahe kila dhambi ambayo watu wanafanya na kila jambo ovu wanlosema

ila kumkufuru Roho Mtakatifu watu hawatasamehewa

Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji. "Mungu hatamsamehe mtu yule amabye anasema mabo maovu dhidi ya Roho Mtakatifu.

Na yeyotte asemaye neno kinyume cha Mwana wa Adamu

Hapa "neno" linamaanisha kile amabcho mtu husema, "N kama mtu atasema chchote kibaya kuhusu Mwana wa Adamu"

Mwana wa Adamu

Yesu anaongea juu yake mwenyewe

hilo atasamahewa

Hili linaweza kuelezwa katikamfumo tendaji. "Mungu atamsamehe mtu kwa ajiloi yahilo"

huyo hatasamehewa

Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji. "Mungu hatamsamehe mtu huyo"

katika ulimwengu huu, na wala ule ujao

Hapa " ulimwengu huu" na " ule ujao" inamaanisha maisha haya ya leo na maisha yajayo. " katika maisha haya au yajayo" au "sasa au baadaye"

Matthew 12:33

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwajibu Mafarisayo

Ama ufanye mti kuwa mzuri na tunda lake kuwa zuri, au uharibu mti na tunda lake

maana yake ni 1) kama utafanya mti kuwa mziri na mtunda yake yatakuwa mazuri na kama ukiuharibu mti na matunda yake yatakuwa mabaya" au 2) "Kama ukiufanya mti kuwa mzuri na mataunda yake yatakuwa mazuri kwa sababu matunda yake ni mazuri na kama ukiyafanya matunda kuwa mabaya yatakuwa kwa sababu matunda yake ni mabaya." Hii ni mithali watu walipaswa kuutumia ukweli kwa jinsi wawezavyo kujua kama mtu ni mbaya au mzuri.

mazuri ... mabaya

"eneye afya ... iliyougua"

mti hutambulika kwa tunda lake

Hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji. "Watu hujua kama mti n mbaya aua mzuri kwa kutazama matunda yake"

ninyi kizazi cha nyoka

Hapa "kizazi" inamaanisha "kuwa na tabia za." Kipiribao ni aina ya nyoka wenye sumu ambao ni hatarina wanawakilisha uovu"

niny ...nyie

Hivi ni viwakilishi vya wingi na vinamaanisha Mafarisayo

mwawezaje kusema mambo mazuri

Yesu anatumia swali kuwakemea Mafarisayo. "huwezi kusema mambo mazuri "Unaweza kusema mambo maovu tu"

kwa kuwa kinywa hunena kutoka katika akiba ya yaliyo moyoni

Hapa "akiba ya moyoni" inamaanisha mawazo ya mtu katika akil iyake. "Kinywa" kinawakilishsa mtu. "Kile ambacho mtu husema katikakinywa chake kinafunua jinsi alivyo katika akili yake"

Mtu mwema katika akiba njema ya moyo wake hutoa wema, na mtu mwovu katika akiba ya uovuwake hutoa kilicho kovu.

Yesu anaongea juu ya "moyo" kama vile kontena lilivyo amablo mtu anaweza kulijaza kwa mambo mazuri au maovu. Hii ni sitiari inayoonesha kile mtu anachosema kinafunua jinsi mtu alivyo.

Matthew 12:36

Sentensi unganishi

Yesu anahitimisha majibu yake hoja za Mafarisayo za kwamba alimponya mtu kwa nguvu za shetani.

Nawaambia

Msisitizo wa kileYesu alichosema baadaye

Watu atatoa hesabu ya kila neno

"Mungu atawauliza watu kuhusu" au "atu watajieleza mbele za Mungu"

Kila neno lililo la maana walilosema

Hapa "neno" inamaanisha kitu ambacho mtu husema. "kila jambo lenye kudhuru watakolokuwa wamesema"

utahesabiwa haki na kwa maneno yako utahukumiwa

Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo tendaji. "Mungu atakuhesabia haki ... Mungu atakuhukumu"

Matthew 12:38

Sentensi unganishi

Maongezi katika mistari hii yananza mara baada tu ya Yesu kujibu hoja za Mafarisayo kwamba alimponya mtu kwa nguvu za shetani

Maelezo kwa ujumla

Katikamstari wa 39, Yesu anaanza kuwakemea waandishi na Mafarisayo

tungependa

"taka"

kuona ishara totka kwako

Unaweza kuiweka wazi kwa nini wanataka kuona ishara "kuona ishara toka kwako ili kuhakikisha kuwa kile unachosema ni kweli.

kizazi kiovu na cha zinaa kinatafua ishara ... itakayotolewa kwao

Yesu anasema na kizazi kilichokuwepo. "ninyi ni waovu na kizazi cha zinaa wanaotafuta ishara toka kwangu ... itakayotolewa kwao

kizazi cha zinaa

Hapa "zinaa" ni sitiari ya watu wasio waaminifu kwa Mungu.

kinatafuta ishara

Ombi hili linamkasirisha Yesu kwa sababu ya mashaka na tabia ya viongozi wa dini juu ya Yesu. Alikuwa amefanya miujiza mingi, lakini bado walikuwa hawamwamini

hakuna ishara itakayotolewa

Hii inaweza kuelezwa katika mmundo tendaji. "Mungu hatawapa ishara"

isipokuwa ile ishara ya nabii Yona

"isipokuwa ishara ileile amabyo Mungu alimpa nabii Yona"

siku tatu mchan nausiku

Hapa "usiku" na "mchana" inamaanisha kipindi cha saa 24 kamili. "siku tatu kamili"

Mwana wa Adamu

Yesu anaongea juu ya yeye mwenyewe

ndani y a moyo wa nchi

Hii inammanisha ndani ya kaburi halisi

Matthew 12:41

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwakemea waandishi na Mafarisayo

Watu wa ninawi

"Raia wa Ninawi"

watasimama mbele ya watu pamoja na kizazi cha watu hawa

"watasimama siku ya hukumu na kuwahukumu kizazi hiki"

Kizazi cha watu hawa

Yesu anamaanisha watu walioishikipindi hiki

watakihukumu

Atakuwa Mungu atayekihukumu kizazi cha watu wa Yesu

na tazama

"na angalia" Hii inatia msisitizo wa kile Yesu alichosema baadaye

mtu fulani mkuu

"mtu wa muhimu sana"

kulikoYona yuko hapa

Unaweza kifanya maana ya sentensi ya Yesu iliyofumbwa kuwa wazi. "kuliko Yona yuko hapa, Lakini bado hamjatubu, hii ndiyo sababu Mungu atawahukumu.

Matthew 12:42

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwakemea waandishi na Mafarisayo

Malkia wa kusini

Hii inamaanisha Malkia wa sheba. Sheba ni nchi iliyo kusini mwa Israeli

atainuka kwenye hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki

"atasimama siku ya hukumu na kuwahukumu watu wa kizazi hiki, Tazama ilivyotafsiriwa katika 12:41

kizazi hiki

Hii inamaanisha watu walioishi wakati Yesu alipokuwa akihubiri

na kukihukumu

Ni Mungu atakayekihukumu kizazi chxa Yesu. "Na Mungu atawasiliza raiawa Ninawi na kukihukumu kizazi hiki "

alikuja toka miishio ya dunia

Hapa "miishio ya dunia" ni nahau inayomaanisha "mbali." Alikuja tokea mbali"

Alikuja

Sentensi hii inaeleza kwa nini Malkia wa kusini atakihukumu kizazi cha Yesu, "allikuja kwa hilo"

na Tazama

"na anagalia" Hii inaongeza msisitizo wa kile Yesu alichosema baadaye

mtu fulani mkuu

"mtu wa muhimu sana"

fulani

Yesu anaongea juu yake

Kuliko Selemani Yuko hapa

Unaweza kuiweka maana ya sentensi ya Yesu iliyofumbwa kuwa wazi. "Kuliko Selemani yuko hapa, lakini hausikilizi. Hiyo ndiyo sababu ya Mungu kuwahukumu"

Matthew 12:43

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwakemea waandishi na Mafarisyao.

Wakati pepo machafu ... kwa kizazi hiki kibovu

Yesu anatumia mfano kuwaonya watu hatari ya kutokuamini

"mahali pasipo na maji

"eneo kavu"au "mahali ambapo watu hawaishi"

lakini hapaoni

Hapa "ni" inamaanisha kupumzika

Kisha husema, 'nitarudi kwenye nyumba yangu niloyotoka

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi na wala si nukuu "kwa hiyo yule roho mchafu huamua kurudi kwenye nyumba yake ambayo alitoka"

kwenye nyumba yangu niliyotoka

Hii ni sitiari ya ya mtu ambaye pepo lilitoka. "pale nilikotoka

arudipo akikuta ile nyumba imesafishwa na iko tayari

Hii inaweza kutafsiriwa katika muunda tendaji. "yule roho mchafu akikuta ile nyumba iko safi na imewekwa kila kitu katika mahali pake",

Hivi ndivyo itavyokuwa kwa kizazi hiki kiovu

Hii inamaanisha kama watu wa kizazi cha Yesu hawatamwamini na kuwa wanfunzi wake, watakuwa katika hali mbaya kuliko walivyokuwa mwanzoni

Matthew 12:46

Maelezo kwa ujumla

Kufika kwa Mama wa Yesu na ndugu zake inakuwa fursa Kwa Yesu kueleza juu ya familia yake ya kiroho

tazama

neno "tazama" lintatuandaakwa ajili ya watu wapya katika simulizi. Lugha yako yaweza kuwa na namna mpya ya kueleza hili

mama yake

Huyu ni Mariamu, Mam wa Yesu wa mwili.

wakitafuta kuongea

"wakitaka kuongea"

mtu mmoja akamwambia, "tazama mama yako na ndugu zako wamesimama nje, wanatafuta kuongea nawe",

Hii inaweza kutafsiriwa kama nukuu isiyo ya moja kwa moja. "mtu mmoja alaimwambia Yesu kuwa mama yake na ndugu zake walikuwa nje na walitaka kuongea naye"

Matthew 12:48

Sentensi unganishi

Huu ni mwisho wa sehemu ya simulizi lililoanzia 12:1 amabapomwadishi ameeleza juu ya kukua kwa upinzani katika huduma ya Yesu

aliyemjulisha

ukweli wa ujumbe ambao yule mtu aliomwambia Yesu unaeleweka na haukurudiwa. "aliyemwambia Yesu kuwa mama yake na ndugu zake walitka kuongea naye"

mamayangu ni nani? na ndugu zangu nu akina nani?

Yesu antumia swali hili kuwafundisha watu. "nitwaambia kweli mamayangu na ndugu zangu ni nani"

Tazama

"anagalia" Hii inatia msisitizo wa kile ambacho Yesu alisema baadaye"

hawa ni mama na ndugu zangu

Hii ni sitiari inayoonesha kuwa wanafunzi wa Yesu ni wake katika familia ya kiroho. Hii ni ya muhimu kuliko kuwa kwenye familia ya kimwili.

yeyote

"mtu yeyote"

baba

Hii ni sifa muhimu ya Yesu

huyo ndiye ndugu yangu, dada yangu na mama yangu

Hii ni sitiari inayomaanisha kuwa wale amabo wanamtii Mungu wanakuwa kwenye familia ya Yesu kiroho. Hii ni muhmu zaidi ya kuwa kwenye familia ya kimwili

Matthew 13

Mathayo13 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri hupendelea kuweka mbele kidogo nukuu za Agano la Kale. ULB na tafsiri nyingine nyingi za Kiingereza huingiza mistari ya 13:14-15, ambayo ni nukuu kutoka Agano la Kale.

Sura hii inaanza sehemu mpya. Ina baadhi ya mifano ya Yesu kuhusu ufalme wa mbinguni.

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Mifano

Mfano ni hadithi fupi inayotumika kuonyesha mfano wa maadili au wa kidini. Katika sura hii, mifano, yanatangaza ukweli kuhusu ufalme wa mbinguni kwa wale ambao wana imani katika Yesu. Pia yanaficha ukweli huo huo kutoka kwa wale wanaomkataa Yesu (Mathayo 13:11-13). Kawaida mifano hii huchukua fomu ya hadithi.

Nahau

Katika sura hii, Yesu anazungumzia macho kuona na masikio kusikia. Anatumia takwimu hizi za matamshi ili kuwahimiza wasikilizaji wake kuelewa masomo ya mifano hiyo.

<< | >>

Matthew 13:1

maelezo ya jumla

Huu nimwanzo wa simulizi jipaya amabapo Yesu anaanza kufundisha makutano, kwa kutumia mifano juu ya ufalme wa mbinguni

katika siku hiyo

Tukio hili liltokea siku hiyohiyo sawa na yale yaliyo kwenye sura iliyopita.

alikaa kando ya bahari

ilimaanisha kuwa alikaa chini kuwafundishsa watu.

aliondoka nyumbani

Haijatajwa kuwa ilikuwa nyumba ya nani ambayo Yesu alikuwa akiishi

aliingia nadni ya mtumbwi

Inamaanisha kuwa Yesu aliingia kwenye mtumbwi kwa sababu ingemfanya iwe rahisi kuwafundisha watu.

mtumbwi

Huu yawezekana mtumbwi wa wazi, uliotengenezwa kwa miti wa kuvulia samaki wenye tanga.

Matthew 13:3

Sentensi unganishi

Yesu anafafanua juu ya ufalme wa mbinguni kwa kutumia mfano wa mpanzi

Yesu alisema maneno mengi kwa mfano

"Yesu aliwaambia maneno mengi kwa mifano"

nao

"kwa wale watu kwenye mkutano"

Tazama

"angalia" au "sikiliza." neno hili linavuta usukivu wa kile Yesu anachotaka kusema baadaye. "uwe tayari kusikiliza jambo amablo nataka kuwaambia"

mpanzi alienda kupanda

"mpanzi alienda kumwaga mbegu shambani"

alipokuwa akipanda

"mpanzi alipokuwa akiendelea kumwaga mbegu"

kandoya njia

Hii inamanisha "njiani wanapopita" peembeni mwa shamba. araidhi ya pale ni ngumu kwa sababu ya watu kuikanyaga.

wakazidonoa

"wakazila mbegu zote"

juu ya mwamba

Hii ni eneo lililojaa miamba na sehemu nyembamba ya udongo ulio juu ya miamba

Ghafla zilichipuka

"zile mbegu zilimea na kukua"

zilichomwa

Hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji. "jua lilichoma ile mimea na ikaungua"

Matthew 13:7

Sentensi unganishi

Yesu anamaliza mfano wa mpanzi

zilianguka katai ya miti ya miiba

"zilianguka mahali ambapo miiba na mimea hukua"

ikaisonga

"ikaisinga ile mimea mipya" tumia neno lako magugu kuzuia mimea mingine kukua vizuri.

kuzaa mbegu

"kuzaa mazao" au "kuzalisha mbegu zaidi" au kutoa matunda"

zingine maramiamoja zadi, zingine sitini, na zingine thelathini

unaweza kuiweka vizuri zaidi katika maana inayoeleweka

mia moja ... sitini ... thelathini

"100 ... 60 ... 30"

aliye na masikio

Hii ni njia inayomaaisha kwa kila anayesikiliza. "Kila anayenisikilza." Tazamaulivyotafsiri katika 11:13

asikie

Hapa "kusikia" inamaanisha kuwa msikivu. "lazima awe makini na kile ninachokisema"

Matthew 13:10

Maelezo kwa ujumla

Yesu anawaeleza wanafunzi wake kwa nini anafundisha kwa kutumia mifano

kwao

Hapa"kwao" inamaanisha wanafunzi wa Yesu

mmepewa upendeleo wa kufahamu siri za ufalme wa mbinguni bali kwao hawajapewa

Hii inaweza kutafasiriwa kwa kutumia muundo tendaji na kutumia taarifa zinazotolewa. " Mungu amewapa fursa ya kuelewa siri za ufalme wa mbinguni" lakini Mungu hajawapa siri hizi watu hawa" au " Mungu amewafnya ninyi kuzielwa siri za ufalme wa mbinguni lakini hajawafanya hawa tayri kuzielewa"

mme

ni kiwakilishi cha wingi kinacho maanisha wanafunzi wa Yesu

siri za ufalme wa mbinguni

Hapa"ufalme" inamaanisha utawala wa Mungu. Kirai"udalme wa mbinguni" kinaonekena kwenye kitabucha mathayo tu. Kama inawezekana jaribu kuiweka katika tafsiri y ako. "siri kuhusu Mungu wetu na utawala wake"

yeyote aliye nacho

"yeyote aliye na ufahamu" au "yeyote anayepokea kile nanachofundisha"

ataongezewa zadi

Hiiinaweza kutafsiriwa katika muundo tendaji. "Mungu atampatia ufahamu zaidi"

ila asiye nacho

"asiye na ufahamu" au " asiyepokea hiki ninachofudisha"

hata kile alicho nacho atanyang'anywa

Hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji. "Mungu atakichukua hata kile alicho nacho"

Matthew 13:13

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwafundisha wanafunzi wake kwa nini anafundisha kwa kutumia mifano

Maelezo kwa ujumla

Katika mstari wa 14 Yesu anamnukuu nabii Isaya ku onyesha kuwa kushindwa kwa watu kuelewa mafundisho ya Yesu ni kutimilika kwa unabii

kwao ... hamta

Viwakilishi vyote vya "kwao" na "hamta" vinamaanisha watu katika kumati.

na ingawawanasikia wasisikie wala kufahamu....

Huu ni mwanzo wa nukuu kutoka kwa nabii Isaya kuhusu watu wasioamini wakatiwa Isaya. Yesu anatumia nukuu hii kuwa kuwaeleza watu waliokuwa wanamsikiliza. Hii ni semi misambamba inayosisitiza kwamba watu walikataakumwani Yesu.

ingawa wanaona, wasione kweli

Matumizi ya pili ya "kuona" hapa yanamaanisha kuelewa.

Ingawa wanasikia wasisike wala kufahamu

Inaweza kuwekwa wazi kwa kile watu wanachosikia. "Ingawa wanasikia kile ninachosema, hawaelewi kile ninachomaanisha.

kwao unabii wa Isaya umetimia ule usemao

Hii inaweza kuelzwa katika mfumo tendaji. "wanatimiza kile Mungu alisema zamani kuptia nabii Isaya"

Msikiapo msikie, lakini kwa namna yeyote hamtaelewa, wakati mwonapo muweze kuona, lakini kwa namna yeyote ile msijue

Huu ni mwanzo wa nukuu kutoka kwa nabii Isaya kwa watu wasioamini wakati wa Isaya. Yesu anatumia nukuu hii kuwaeleza watu waliokuwa wanamsikiliza. Hii ni misemo sambamba inayosisitiza kuwa watu walikataa kuuelewa ukweli wa Mungu.

msikiapo msikie lakini kwa namna yeyeote msiweze kuelewa.

"mtaskia vitu lakini hamtavielewa" unaweza kuviweka wazi kile amabcho watu watasikia. "Mtasikia kile Mungu asemacho kupitia nabii lakini hamtaelewa maana halisi"

wakati mwonapo muweze kuona lakini kwa namna yeyote msiweze kuelewa

Unaweza kuweka wazi kile ambacho watu wataona. "mtaona kile amabcho Mungu anafanya kupitia nabii, lakini hamtaelewa"

Matthew 13:15

Sentens iunganishi

Yesu anamaliza kumnukuu Isaya

Na mioyo ya watu hawa ... ningewaponya

Ktika 13:15 Mungu anawaeleza watu wa Israwli kana kwamba ni wenya ugonjwa wa mwili ambao unawafanya wasiweze kuelewa, kuona na kusikia Mungu anawataka waje kwake ili awaponye.

Mioyo ya watu hawa imekuwa giza

Mioyo inamaanisha akili. "mioyo yao imekuwa migumu kujifunza"

ni vigumu kusika

wao si viziwa wa masikioya mwili 'vigumu kusikia"wanakataa kusika na kujifunza ukweli wa Mungu

wamefumba macho yao

hawajafumba macho yao ya mwaili. hii inamaanisha hawataki kuelewa.

ili wasiweze kuona kwa macho yao au kusikia kwa masikkio yao auakuelewa kwa mioyo yao, hivyo wangenigeukia tena.

"ili kwamba wasiweze kuona kwa macho yao, kusikia kwa masiko yao, au kuelewa kwa mioyo yao amabyo matokeo yake ni kumrudia Mungu.

wangenigeukia

"kugeukia kwangu tena" au "kutubu"

ningewaponya

"mimi ningewaponya" Hii inamaanisha Mungu angewaponya kiroho kwa kuwasamehe makosa yao na kuwapokea tena kama awatu wake.

Matthew 13:16

Sentensi unganishi

Yesu anamaliza kuongea na wanafyunzi wake kwa nini anaongea nao kwa mifano

Bali macho yenu yameberikiwa kwa kuwa yanaona, na masikio yenu, kwa kuwa yanasikia

Sentensi zote zina maanisha kitu kilekile. Yesu anasisitiza kuwa wamempendeza kwa sababu wameamini kile ambacho Yesu amesema na wamefanya.

Bali macho yenuyamebarikiwa kwa kuwa yanaona

macho yanamaanisha nafsi kamili. mmebarikiwa kwa sababu machoyenu yanaweza kuona

Yenu .. wewe

viwakilishi hivi ni vya wingi

na masikio yenu, kwa vile yanaona

masikio yanmaanisha nafsi kamili

hakika nawambia

"nawambia ukweli" hii inaongeza msisitizo kwa kile anlichosema Yesu baadaye.

mamabo mnayoyaona

Unaweza kuyaweka wazi yale waliyoyaona "Yle mambo uliyoyaona mimi nikfanya

mambo uliyoyasikia

mambo uliyosikia mimi nikisema

Matthew 13:18

sentensi unganishi

Yesu anaanza kufafanua kwa wanafunzi wake ule mfano wa mpanzi unaoanzi 13:3

neno la ufalme

neno linamaanisha ujumbe "ufalme" unamaanisha utawala wa Mungu kama mfalme

mwovu huja nakukinyakua kilichokwisha kupandwa mioyoni mwenu

Yesu anaongea juu ya shaetani anayewafanya kusahau kile walichosikia kama ndege anavyozidonoa mbegu zilizoanguka chini.

mwovu

shetani

kukinyakua

kukichukua kitu kwa mtu aliyesahihi

kilichokwishapandwa ndani ya moyo wake

ujume ule Mungu aliopanda nadani ya moyo wake.

ndani ya moyo ake

moyo unamanisha akili ya msikilizaji

hii ni mbegu iliyopandwa kando ya njia

tafsiri kama ilivyo 13:3

Matthew 13:20

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kwaeleza wanafunzi wake mfano wa mpanzi

yeye aliyepandwa katika miamba

"kilichopandwa" kinamaanisha mbegu iliyoanguka kwenye miamba.

Kilichopandwa kwenye miamba ni

miamba ambapo mbegu zilianguka inmaanisha udongo uliokuwa juu ya miamba ambapo mbegu zilianguka

yule asikiaye neno

katika mfano, mbegu zinamaanisha neno

neno

ujumbe wa Muungu

hulipokea kwa furaha

kulipokea neno kwa furaha

ila hana mizizi ndani yake hiyo huvumilia kwa kitambo kifupi.

mizizi inamaanisha kile kinachomfanya mtu aendelee kuamini ujumbe wa Mungu

hujikwaa ghafla

kujikwaa humaanisha kuacha kuamini ujumbe wa Mungu

Matthew 13:22

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwawleza wanafunziwake kuhusu mfano wa mpanzi

aliyepandwa

hii ni mbegu iliyopandwa au iliyoanguka

iliyopandwa kati ya miiba

ardhi ilyo na miiba amabapo mbegu ilipandwa

huyu ni yule

inamaanisha mtu

neno

inaanisha ujumbe wa Mungu

masumbuko ya ulimwengu na udanganyifu wa utajiri hulisonga lile nenoi

Yesu anaongelea masumbufu ya ulimwengu na udanganyifu wa utajiri hugeuza nia ya mtu na kushindwa kutii neno la Mungu kama vile magugu yanavyoweza kuuelemea mmea na kushindwa kukua.

masumbko ya ulimwengu

"mamabo ya dunia ambayo huwafanyawatu wawe na mashaka

udanganyifu wa utajiri

Yesu anautumia utajiri kama mtu adanganyaye watu. Hii inamaanisha kuwa watu hudhani kuwa na pesa nyingi huwafanya kuwa na furaha, lakini si kweli.

lisije likazaa matunda

kutokuzaa matunda

aliyepandwa kwenye udongo mzuri

kwenye udongo mzuri ambapo mbegu zilipandwa

azaaye matunda na kuendela kuzaa

Hapa mtu amefananishwa na mti uzaao. "Kama mti wenye afya uzaoa matunda, ambaye ni mzalishaji.

kuzaa moja zaidi ya mara mia, nyingine sitini, nyingine thelatiini

watu wengine huzalisha 100 mara, wengine 60 na wengine 30.

Matthew 13:24

Sentensi unganishi

Hapa Yesu anaelezea juu ya uafalme wa mbinguni kwa kutumia mfanao wa shamba lilikuwa na ngano na magugu vikikuwa pamoja

Ufalme wa mbinguni umefananishwa

tafasiri islinganishe ufame wa mbinguni na mtu, bali ufalme wa mbinguni kama ulivyoelezwa kwenye mfano.

ufalme wa mbinguni umefananishwana mtu

"Wakti Mungu wa mbinguni atakapojionesha kama mfalme"

ufalme wa mbinguni umefananishwa n

wakati Mungu wetu wa mbinguni atakapojidhirisha kama mfalme, itkuwa kama

mbegu nzuri

"mbegu nzuru ya chakula" au "nafaka nzuri"

adaui ake akaja

"adaui wake akaja shambani"

magugu

magugu huonekena kama mimea ya chakula yanapokuwa hayajakomaa. laini mbegu zake huwa nasumu" au "mbegu mbaya" au mbegu za magugu"

baadaye ngano ilipoota

"badaye mbegu za ngano zilipoota" au "wakati mimea ilipochipua"

ilipotoa mazao

"ilipotoa nafaka" au "ilipotoa mbegu za ngano"

ndipo magugu yalitokea pia

"watu waliweza kuyaona magugu shambani pia"

Matthew 13:27

Sentensi ungsnishi

Yesu anaendelea kueleza mfano wa magaugu na ngano kukua kwa pamoja katika shamba

mwenye shamba

huyu ndiye aliyepanda mbegu nzuri shambani

Haukupanda mbegunzuri katika shamba lako?

ulipanda mbegu nzuri katika shamba

je, haukupanda

tulipanda

akawaambia

"mwenye shamba akawaambia watumishi"

kwa hiyo unatutaka

kiwakilishi "tu" kinamaanisha watumishi

Matthew 13:29

Sentensi unganishi

Yesu anahitimishas mfano wa magugu yalyokua pamaoja na ngano shambani

Mwenye shamba akasema

"Mwenye shamba akasema kwa watumishi"

nitasema kwa wavunaji, 'kwanza yang'oeni magugu na yafungeni matita matita na kuyachoma, lakini kusanyeni ngano katika ghala langu,"

"Nitawaambia wavunaji kwanza kuyakusanya magugu na kuyafunga matita matita na kuyachoma, kisha kusanyeni ngano katika ghala langu"

ghala

Jengo la shambani ambalo lilitumika kwa kukusanyia nafaka.

Matthew 13:31

Esntensi ungsnishi

Yesu anaufafanua ufalme wa mbinguni kwa kutumia mfano wa mbegu ambayo hukua na kuwa mti mkubwa

Ufalme wa mbinguni unafanana n a

"Wakati Mungu wetu wa mbinguni atakapojidhihirisha kama mfalme kuwa mfalme, itakuwa kama", Tazama 13:24.

mbegu ya haradari

ni mbegu ndogo sana ambayo huweza kukua na kuwa mti mkubwa

Mbegu hii kwa hakika ni ndogo kuliko mbegu zingine zote

Mbegu za haradari zilikuwa mbegu ndogo zadi ambazo zilifahamika kwa wasikilizaji wa kwanza

Lakini imeapo

"Lakini mmea unapokuwa"

huwa kubwa kuliko

ni mkubwa kuliko

huwa mti

Mmea wa haradli hukua kiasi cha mita 2 had 4 za urefu

ndege awa angani

"ndege"

Matthew 13:33

Sentensi unganishi

Yesu anaelezea ufalme wa mbinguni kwa kutumia mfano wa chahu na jinsi inavyoweza kuufanya udongo

Ufalme wa mbinguni ni kama chachu

Ufalme si kama chachu, lakini kusambaa kwa ufalme ni kama kusambaa kwa chachu

ufalme wa mbinguni ni kama

ufalme wa mbinguni una, maanisha utawala wa Mungu kama mfalme..Kirai "ufalme wa mbinguni" kimetumika katika Mthayo tu. Mungu wetuwa mbinguni atakapojidhihirisha kama mfalme itakuwa kama"

vipimo vitatu kwa unga

"kipimo kikubwa cha unga" au tumia kipimo kinachotumika katika utamaduni wako cha kuonesha kipimo kikubwa cha unga.

mpaka viumuke

Maana kusudiwa hpa ni kwamba, chachu na vile vipimo vitatu vya unga vilitengenezwa kwa ajiliya kuumulia.

Matthew 13:34

Maelezo kwa umumla

Mwandishi anannukuu toka Zaburi kuonesha kuwa mafundisho ya Yesu kwa mfano ni kwa ajili kutimiza unabii

Hayo yote Yesu aliyasema kwa mifano, Na pasipo mifano hakusema chochote kwao

Sentensi zote zina maana moja. Zimeunganishwa kusisitiza kwamba Yesu alifundisha makutano kwa kutumia mifano.

hayo yote

Hii inamaanisha kuwa kile alichofundisha Yesu kinaanzia 13"1

Pasipo mifano hakusema chochote kwao

""hakufundisha chochote isipokuwa kwa mifano"

kile kilichokwisha semwa kupitia kwa nabii kiweze kutimia, pale aliposema

alaikifanya kiwe kweli kile alichokuwa amemwambia mmoja wa manabii kukiandika hapo zamani

aliposema

nabii aliposema

nitafumbua kinywa chcangu

Hii ni nahau inayomaanisha kuwa nitasema "nitasema"

yaliyokuwa yamefichwa

mambo ambayo Mungu ameyaficha

tangu misingi ya ulimwengu

"tangu kuanza kwa ulimwengu" au tangu Mungu aumbe ulimwengu"

Matthew 13:36

Sentensi ungnishi

Mandhari yanahamia kwenye nyumba amabyo Yesu na wanafunzi wake walikuwa wanaishi. Yesu anaanza kuwafundiasha mfano wa shamba ambalo lilikuwa na magugu na ngano alilokuwa amewaambia mwanzoni katika 13:24.

kwenda nyumbani

"aliingia ndani" au "aliingia kwenye nyumba ile aliyokuwa anaishi"

apandae

"mpamzi"

Mwana wa Adamu

Yesu anamaanisha yeye mwenyewe

wana wa ufalme

Hapa "wana wa" inamaanisha kuwa mali ya au kuwa na tabia zilezile alizo nazo.

wa ufalme

Mungu ni mfalme

wana wa yule mwovu

watu ambao ni mali ya yule mwovu

adui aliyezipanda

"adui aliyepanda magugu"

mwisho wa ulimwengu

"mwisho wa nyakati

Matthew 13:40

Sentensi unganishi

Yesu anamaliza kuwaeleza wanafunzi wake mfano wa shamba lenye magugu na ngano

Kama vile magugu yanavyokusanywa nakuchomwa moto

Kwa hiyo, kama watu wayakusanyavyo magugu na kuyachoma moto"

mwisho wa ulimwengu

mwisho wa nyakati

Mwana wa Adamu atawatuma malaika zake

Yesu anamaanisha yeye mwenyewe

wale watendao maasi

"wale wasio na sheria" au "watu waovu"

tanuru la moto

moto wa kuzimu

kulia nakusaga meno

Hii inamaanisha huzuni kubwa na mateso

watakapong'aa kama jua

watakuwa rahisi kuwaona kama jua

Baba

hiki ni cheo muhimu cha Mungu

yeye aliye na masikio

kila anayenisikiliza

Matthew 13:44

Sentensi unganishi

Yesu anaelezea juu y a ufalme wa Mungu kwa kutumia mifano miwili ya watu waliouza mali zao kwa kununua kitu cha thamani zaidi

Maelezo kwa ujumla

Katika mifano hii Yesu anatumia milinganyo miwili kuwafundisha wanfanzi wake kuhusu mfano wa ufalme wa mbinguni

Ufalme wa mbinguni ni kama

Tazama ilivyotafsiriwa katika 13:24

kama hazina iliyofichwa shambani

hazina ambayo mtu alificha shambani

hazina

kkitu cha thamani sana au vitu vilivyokusanywa

kuficha

alifunika kwa juu

aliuza kila kitu alichokuwa nacho na kulinunua shamba lile

Maana yake nin kwamba yule mtu ananunua lile shamba ili ili achukue ile hazina iliyofichwa

ni kama mtu anayefanya biashara atafutaye lulu ya thamani

maana yake ni kwamba yule mtu alikuwa anatafuta ile luu ya thamani ili aweze kuinunua

mfanya biashara

mchuuzaji au mtu anayeshughulika kuuza vitu vya jumla ambaye mara kwa mara hupata wateaja tokea mbali

lulu ya tahmani

"lulu" ni kitu lain, kigumu, kinachong'aa, cheupe au shanga yenye mng'ao inayopatikana kwenye viumbe wenye asili ya konokono baharini. Lulu ina bei y a juu sana na hutengenezwa vitu vya thamani kama pete.

Matthew 13:47

Sentensi unganishi

Yesu anaelezea ufalme wa mbinguni kwa kutumia mfano wa mvuvi anayetumia nyavu kubwa kukamata samaki

Ufalme wa mbinguni ni kama nyavu

ufalme sikama nyavu, lakini ufalme hukokota watu wa kila aina kamavile nyavu zikokotavyo aina zote za samaki

ufalme wa mbinguni ni kama

tazama katika 13:24

ni kama nyavu iliyo ndani ya bahari

kama nyavu ambayo wavuvi hutupa ndani ya bahari

iliyotupwa ndani ya bahari

"iliyotupwa baharini"

hukusanya viumbe wa kila aina

"ilikamata viumbe wa kila aina

walivuta ufukweni

"walivuta ule wavu mpaka ufukweni"

vitu vyema

"vile vizuri"

visivyo na thamani

"samaki wabaya" au "samaki wasiofaa"

vilitupwa mbali

"havikutunzwa"

Matthew 13:49

Sentensi unganishi

Yesu anaeleza mfano wa mvuvi aliyetumia wavu mkubwa kukamata samaki

mwisho wa dunia

"mwisho wa nyakati"

watakuja

"kuja" au "kwenda" au "kuja toka mbinguni"

watu waovu kutoka miongoni mwa wenye haki

watu waovu kutoka miongoni mwa wenye haki"

na kuwatupa

"malaika watawatupa watu waovu"

tanuru ya moto

tazama 13:40

maombolezo na kusaga meno

Tazama 8:11

Matthew 13:51

Sentensi unganishi

Yesu anaeleza ufalme wa mbinguni kwa kueleza mfano wa mtu anayewatawala watumishi wa nyumbani.Huu ni mwisho wa habari ya Yesu kuwafundisha watu kuhusu ufalme wa mbinguni kwa kutumia mifano

Mmefahamu mambo yote haya? wanafunzi walimjibu, "Ndiyo"

Yesu aliwaulizakamawalikuwa wameelewa yote haya, na walisema kwamba walielwa

amakuwa mwanafunzi wa ufalme wa mbingun

amaejifunza ukweli kuhusu Mungu wetu wa mbinguni ambaye ni mfalme.

unafananan na mwenye nyumba ataoaye katika hazina yake vitu vipya.

Yesu anafundisha mfano mwingine. Anawafananisha waandishi, ambao wanalyafahamu maandiko vizuri ambayo Musa na manabii waliandika, na ambao pia sasa wanayapokea mafundisho ya Yesu na kuyalinganisha namwenye nyumba anayetumia vitu hazina ya zamani na mpaya.

hazina

Hazina ni kitu cha thamani. Hapa panafananishwa na mahali ambapo vitu huhifadhiwa. "chumba cha kutunzia".

Ikawa Yesu alipomaliza

Kirai hiki kinatuhamishaia simulizi yetu ya mafundisho ya Yesu kwenda kile kilichotokea baadaye.

Matthew 13:54

Maelezo kwa ujumla

Huu ni mwanzo wa habari mpya inyotupeleka hadi 17:26, ambapo mwandishi anaeleza juu ya mwendelezo wa upinzani katika huduma ya Yesu kuhusu ufalme wa mbinguni. Hapa watu wa nyumbani kwao Yesu wanamkataa..

"mji wa nyumbani kwao

" Huu ni mji wa Nazarethi ambapo Yesu alikulia

katika masinagogi yao

kiwakilishi "yao" kinamaanisha watu wa eneo hilo

walishangaa

"walishangaa

Ni wapi mtu huyu alipopata hekima hii na miujiza

"Yawezekananje mtu wa kawaida kama huyu kuwa na mwenye hekima na kufanya miujiza mikubwa.

Mtu hyu siyo mwana wa seremala ...ameyapata wapi haya yote.

Makutano wanatumia maswali haya, kuonyesha mshangao wao kuwa mtu wa kawaida kutoka mji wao anafanya mambo haya yote. Mtu wa kawaida hawezi kuyafanaya haya yote.

Matthew 13:57

Aliwachukiza

watu walimkataa Yesu

Nabii hakosi kuwa na heshima isipokuwa kwao

nabii hupokea heshima kila mahli

nchini yao

"mji wa kwao"

kwao

"nyumbani kwao"

Na hakuweza kufanya miujiza mingi

"Yesu hakuweza kufanya miujiza nyumbani kwao"

Matthew 14

Mathayo14 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

14:3-12 inataja matukio yaliyotokea hapo awali. Kwa hiyo, kuna mkatizo katika utaratibu wa matukio wa hadithi. Kusudi la mkatizo huu ni ufafanuzi; mtafsiri ataona umuhimu wa kuashiria mkatizo huu.

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Kinaya

Herode aliamini kwamba kuvunja kiapo kulikuwa na aibu, hivyo aliamuru kuuawa kwa Yohana Mbatizaji. Hata hivyo, mauaji ambayo aliwajibika ilikuwa mbaya zaidi. Hii ni kinaya. (Angalia: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-irony)

<< | >>

Matthew 14:1

Maelezo kwa ujumla

Mistari hii inaeleza jinsi Herode alivyopokea aliposikia habari za Yesu. Tukio hili linfuatia baada ya tukio linalofuata katika simulizi

Kwa wakati huo

"Katika siku hizo" au "wakati Yesu akiendelea na huduma huko Galilaya"

alaisikia habari juuya Yesu

alaisikia juu ya uvumi wa Yesu

Akawaambia

"Herode alisema"

amaefufuka ktoka wafu

amerudi kuishi

kwa hiyo nguvu hizi zipo juu yake

Baadhi ya Wayahudi waliamini kuwa kama mtu atarudikutoka wafu anaweza kuwa nanguvu za kufanya mambo makubwa.

Matthew 14:3

Sentensi unganishi

Hapa mwandishi anaanza kueleza jinsi Herode alivyomnyonga Yohana mbatizaji. Matukio haya yanaanza kuonekana kabal y a matukio yaliyo kwenye mistari iliyopita

Maelezo kwa ujumla

Mwandishi anaeleza upya habari ya kifo cha Yohana mbatizaji ili kuonesha kwa nini Herode aliitikia kwa jinsi alivyofanya aliposikia habari za Yesu

Kwa kuwa Herode .... kuwa mke wako

Kama inahitajika unaweza kurudia mpangilio wa tukio kama ulivyo 9:3 -4.

Herode alikuwa amemkamata Yohana na kumfunga, na kumtupa gerezani

Inasemekana kuwa Herode alifanya mabo haya kwa sababu aliwaamuru wengine kufanya kwa ajili yake.

mke wa Filipo

Filipo ni jina la kakawa Herode

Kwa kuwa Yohana alimwambia kuwa si halali kumchukua yeye kuwa mke wako

Kwa kuwa Yohana alikuwa amemwambia kuwa siahali kwake kumchukua kama mke wake"

kwa kuwa Yohana alimwambia

"Kwa kuwa Yohana aliendelea kumwambia Herode"

si halali

Filipo bado alikuwa hai wakati Herode anamwoa Herodia

aliogopa

Herode aliogopa

walimwona

"walimwona Yohana

Matthew 14:6

katkati ya watu

katikati ya wageni waliokuwa wamehudhuria ile sherehe ya kuzaliwa

Matthew 14:8

Baada ya kushauriwa na mama yake

baada ya mama yake kumpa maelekezo

kumwelekeza

"kumfundisha" au "kumwambia"

alisema

"binti wa Herodia alaisema kwa Herode"

kombe

sahani kubwa sana

mfalme alikuwa na sikitiko

ombilake lilimfanya mfalme asikitike

mfalme

"mfalme Herode"

aliamuru kwamba inapaswa ifanyike

"aliwaamuru watu wake wafanye alichosema"

Matthew 14:10

Sentensi unganishi

Hii inakamilisha habari ya Herode alivyomuua Yohana mbatizaji

kichwa chake kikaletwa juu ya sinia na akapewa binti

mtu mmoja akaleta kichwa chake kwenye sinia akpeewa yule binti

sinia

sahani kubwa sana

binti

binti ambaye hajaolewa

wanafunzi wake

wanafunzi wa Yohana

mwili

maiti

walienda kumwambia Yesu

wanafunzi wa Yohana walienda kumwambia Yesu kile kilichotokea kwa Yohana mbatizaji

Matthew 14:13

Sentensi unganishi

Mistari hii inaeleza jinsi Yesu alivyopokea taarifa za kuuawa kwa Yohana mbatizaji.

Maelezo kwa ujumla

Mistari hii inatoa historia yaju ya muujiza ambao Yesu anataka kuufanya wa kulisha watu elfu tano.

Naye

Neno hili limetumika hapa kama mwanzo wa habari mpya. Hapa Mathayo anaanza kueleza sehemu mpya ya habari hii.

ulipofahamu

" walposika kilichoteka kwa Yohana au waliposikia habari za Yohana

akajitenga

"aliondoka" au "alaienda mbali n a kundi

kutoka mahali pale

"kutoka eneo hilo"

wakati umati ulipofahamu

"wakati umati waliposikia kule Yesu alikokuwa ameenda

umati

"makutano ya watu" aua "kundi kubwa la watu"

kwa miguu

Hii inamaanisha kuwa wale watu walikuwa wkitembea

kisha Yesualikuja mbele zao akauona umati

Yesu alipokuja karibu na ufukwe akauona umati wa watu

Matthew 14:15

Sentensi unganishi

Hii inaanzisha habari ya Yesu akiwalisha watu elfu tano kwa mikate mitano na samaki wawili

wanafunzi wakaja kwake

"wanafunzi wa Yesu wakaja kwake"

Matthew 14:16

hawana haja

"watu hawana haja"

wapeni ninyi

neno "ninyi" ni la wingi linalomaanisha wanafunzi

wakamwambia

"wanafunzi wakamwambia Yesu

mikate mitano

mkate ni bonge lenye sura kama donge lililookwa

"ileteni kwangu"

"leteni mkate na samaki kwangu

Matthew 14:19

Sentensi unganishi

Hii inahitimisha habari ya Yesu ya kuwalisha watu elfu tano

kukaa chini

kaeni

akachukua

akabeba mikononi mwake

kumega mikate

kuivunja mikate

mikate

mikate mizima

akatazama juu

maana zaweza kuwa 1) alipokuwa akitazama juu 2) baada ya kutazama juu

wakala wote na kushiba

walishiba hadi walipokuwa hawana njaa

walikusanya

wanafunzi walikusanya aua waaaaatu walikusanya

vikapu kumi na mbili

vikapu 12 vilivyojaa

waliokula

waliokula mikate na samaki

elfu tano

wanaume 5,000

Matthew 14:22

Sentensi unganishi

Mistari ifuatayo inaelaza matukio yaliyotokea baada ya Yesu kuwalisha watu elfu tano

Maelezo kwa ujumla

Mistari hii inatoa historia juu ya muujiza amabo Yesu anataka kuuonesha juu ya kutumbea juu ya maji

Mara moja

"Punde tu baada ya Yesu kuwalisha watu wote"

ilipokuwa jioni

"baadaye jioni" au "giza lilipoingia"

bahari ikiyumbayumba kwa sababu ya mawimbi

"na wanafunzi hahawezi kuiongoza mashua kwa sababu ya mawimbi makubwa"

kwani upepo ulikuwa wa mbisho

kwani upepo ulivuma kinyume nao

Matthew 14:25

zamu ya nne

zamu ya inne ilikuwa kati ya saa 9 za usiku mpaka machweo

akaitembea juu ya bahari

akaitembea juu ya maji

walihofu

"waliogopa sana

Ni mzuka

Roho ile iliyotengana na mwili wa mtu baada ya kifo

Matthew 14:28

Petro alimjibu

Petro alimjibuYesu

Lakini Petro alipoona mawimbi

Hapa "kuona mawimbki" maana yake ni kwamba ni kwamba alitambua kuwa kulikuwa na upepo

Matthew 14:31

wewe mwenye imani ndogo

"wewe uliye na imani ndogo kiasi hicho

kwa nini ulikuwa na mashaka

Haukupaswa kuwa na mashaka

Mwana wa Mungu

Hii ni sifa ya muhimu ya Yesu inayoonesha mahusiano kati yake na Mungu

Matthew 14:34

Sentensi unganishi

Mistari hii inaeelza kile kilichotokea baada ya Yesu kutembea juu ya maji. Mistari hii inatoa muhtasari wa jinsi watu walivyokuwa wakiitikia kwenye huduma ya Yesu

Na walipokwisha kuvuka

Wakati Yesu na wanafunzi walipokuwa wamevuka bahari

Genesareti

Huu ni mji mdogo ulioko Kaskazini Magharibi mwa mji wa bahari ya Galilaya

walituma ujumbe

"wanaume wa eneohilo waltuma ujumbe

walmsihi

waagonjwa walimsihi

Pindo la vazi lake

"chini yavazi" au "ncha ya vazi"

vazi

"joho" au "kile alichokuwa amevaa"

waliponywa

wakawa salama

Matthew 15

Mathayo15 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri hupendelea kuweka mbele kidogo nukuu za Agano la Kale. ULB na tafsiri nyingine nyingi za Kiingereza huingiza mistari yote ya 15: 8-9, ambayo ni nukuu kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

"Desturi"

"Desturi za wazee," yaani, sheria zilizotamkwa, ni dhana muhimu katika sura hii. Hizi ndizo sheria ambazo viongozi wa kidini kati ya Wayahudi walikuza ili kuhakikisha kwamba Sheria ya Musa ilipata utii. Hata hivyo, sheria hizi mara nyingi zilikuwa muhimu zaidi katika vitendo kuliko Sheria ya Musa yenyewe. Yesu aliwakemea viongozi wa kidini kwa hili, na kwa sababu hiyo wao wakawa na hasira. (Angalia: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lawofmoses)

Wayahudi na Wayunani

Imani ya mwanamke Mkanaani kwake Yesu ulikuwa tofauti sana na kutomkubali kwa viongozi wa Kiyahudi. Tofauti hii ilichangia kukemewa vikali kwa viongozi hao.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Kondoo

Watu mara nyingi huashiriwa kama kondoo katika maandiko. Katika sura hii, taswira ya kondoo inaonyesha kuwa Wayahudi walikuwa wamepotea kiroho bila ya kuwa na kiongozi mwafaka wa kuwaongoza.

<< | >>

Matthew 15:1

Maelezo kw ujumla

Hapa Yesu anajibu hoja za Wayahudi

kwa nini wanafunzi wanayahalifu mapokeo ya wazee?

wanafunzi wako hawaziheshimu taratibu amabzo mababu zetu walitupa

Mapokeo ya wazee

Hizi si sawa na sheria za Musa. haya ni mafundisho na tafsiri za sheria zilizotolewa na viongozi wa dini baada ya Musa

hawanawi mikono y ao

kunawa huku siyo tu kwa kusafisha mikono. Hii inamaanisha kunawa kwa desturi kutokana na taratibu za wazee. Hawaoshi mikono yao vizuri

Nanyi kwa nini mnaihalfu sheri ya Bwana kwa ajili ya mapokeo yenu

Nami n aona kwamba mnakataa kuzitii sheria za Mungu ili tu mweze kufuata kile ambacho mababu zenu waliwafundisha

Matthew 15:4

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kwajibu Mafarisayo

Maelezo kwa ujumla

Katika mstariwa 4, Yesu ananukuu m ara mbili kutoka kitabu cha kutoka ili kuonyesha jinsi Mungu anavyotegemea watu kuwatendea wazazi wao

hakika atakufa

watu watamuua

Lakini ninyio husema, 'kila amwambiaye baba yake na mama yake ... mtu huyo hana haja ya kumheshimu baba yake

Lakini mnafundisha kuwa mtu hahitajio kuwaheshimu wazazi wake kwa kuwapa kitu ambacho kingeweza kuwasaidia kama mtu atawaambia wazazi wake hivyo tayari ameto zawadi kwa Mungu

hana haja ya kumheshimu baba yake

inamaanisha kuwa baba yake ni mzazi wake. Hii inamaanisha kuwa viongozi wa dini waliwafundisha kuwa mtu hana haja ya kumheshimu mzazi wake kwa kumsaidia.

mmelitangua neno la Mungu kwa ajiliya mapkeo yanu

Mmezifanya desturi zenu kuwa za muhimu kulikko neno la Mungu

Matthew 15:7

Sentensi unganishi

Yesu anahitimisha majibu yake kwa Mafarisayo

Maelezo kwa ujumla

Katika mstari wa 8 na 9Yesu anamnukuu nabii Isaya kwa kuwakemea Mafarisayo na waandishi

ni vyema kama Isaya alivyotabiri juu yenu

Isaya alisema ukweli katika unabii wake juu ayenu

alaposema

aliposema kile ambacho Mungu alisema

watu hawa wananiheshimu mimi kwa midomo yao

Watu hawa wanasema kweli kwangu

kwangu

viwakilishi vya "kwang"u vinaanisha Mungu

lakini mioyo yaoiko mbali na mimi

watu hawjajitoa kwa ukweli kwa Mungu

wananiabudu bure

"Ibaada zao hazina maana kwangu" au "wanaigiza kuniabudu mimi"

maagizo ya wanadanu

"shseria ambazo watu hutengeneza

Matthew 15:10

Sentensi unganishi

Yesu anaanza kuwafundisha makutano na wanafunzi wake juu ya kile kinachomtia mtu unajisi na kwa nini mMafarisayo na waandishi walikuwa wamekosea kumkosoa Yesu

Sikilizeni na mfahamu

Sikilizeni kwa makini kile ninachosema ili muelewe maana yake.

Kiingiacho mdomono ... kitokacho kinywani

Yesu anatofautisha kile ambacho mtu hula na kile asemacho. Yesu anamaanisha kuwa Mungu hujali zaidikile ambacho mtu husema kuliko kile ambacho hula

Matthew 15:12

Mafaaarisayo walipolisikia lile neno walikwazika

Usemi huu uliwafanya Mafarisayo wachukie

Kila mmea ambao baba yangu wa mbinguni hajaupanda utang'olewa

Hiki ni kirai kinachomaanisha kuwa Mafarisayo si watu wa Mungu, kwa hiyo Mungu atawatoa

Baba yangu wa mbinguni

Hiki ni cheo cha Yesu kinachoonesha uhusiano kati yake na Mungu

watang'olewa

Baba yangu atawang'oa

waacheni pekee

neno pekee linamaanisha Mafrarisayo

mtu kipofu ... wataanguka shimoni

Inamaanisha kuwa Mafarisayo hawajui amari za Mungu au jinsi ya kumpendeza Mungu Kwa hiyo, hawawezi kuwafundisha wengine jinsi ya kumpendeza Mungu

Matthew 15:15

Sentensi unganishi

Yesu anaeleza mfano amabao amefundisha katika 15:12

kwetu

kwetu wanafunzi

bado hamuelewi

Yesu mfano kuwakemea wanafunzi kwa kutokuelewa mfano. Pia kwakilisha cha "hamu" kimesisitizwa. Yesu hawezi kuwaamini wanafunzi wake kwa kutokuelewa. Nimekatishwa tamaa na ninyi wanafunzi wangu kwa kuwa hamjaelewa kile ninachofundisha.

Nanyi hamuoni kuwa kile kiendacho ... na kwenda chooni

Yesu anatumia swli kuwakemea wanafunzi kwa kutokuelewa mfano. "hakika mnaelewa ... kwenda chooni"

kiendacho mdomoni

hupitia mdomoni

chooni

Hii ni tafsida kwa eneo ambalo watu huzika uchafu wa mwili

Matthew 15:18

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kufundisha mfano aliofundisha katika 15:12

vyote vitokavyo mdomoni

Hii inamaanisha kile ambacho mtu husema

katika moyo

Hapa "moyo" inamaanisha akili za mtu au ndani ya mtu.

uuaji

kuua mtu asiye na kosa

ushuhuda wa uongo

Kusema kitu juu ya mtu mwingine ambacho ni cha kuumiza na si cha kweli

bila kunawa mikono

Hii inamaansha mtu ambaye hajaosha mikono kwa desturi za wazee

Matthew 15:21

Maelezo kwa ujumla

Hii inaazisha habari y aYesu kumponya binti wa mwanamke Mkananayo

Yesu akatoka

Inamaanisha kuwa wanafunzi waliondoka na Yesu

Tazama, akaja mwanmke Mkanani

Kulikuwa na mwanamke Mkanaani aliyekuja kwa Yesu

Akaja mwanamke Mkanaani kutoka pande hizo

"mwanamke kutoka kundi la watu aliyeitw Mkaanani anayeishi katika eneo hilo.

Nihurumie

Kirai hiki kinamaanisha kuwa alikuwa akimuomba Yesu amponye binti yake.

Mwana wa Daudi

Yesu hakuwa Mwana wa Daudi kimwili, hii inaweza kutafsiriwa kama "wa kizazi cha Daudi"

binti yangu anateswa sana na pepo

Pepo linamtesa sana binti yangu

lakini Yesu hakumjibu neno

Hapa "neno" linamaanisha kile mtu asemacho

Matthew 15:24

Sikutumwa kwa mtu yeyote

Mungu hakunituma kwa yeyote

isipokuwa kwa kondoo waliopotea

Tazama 10:5

alaikuja

mwanamke Mkanaani alikuja

akainama

Hii inaonesha kuwa yule mwanake alikuwa akinyeynyekeza mbele za Yesu

Siyo vyema kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa

Yesu anamjibu mwanamke kwa kutumia mithali. Maana yake ni kwamba siyo sawa kuchukua kitu cha Wayahudi n a kuwapa watu wasio kuwa Wayahudi.

mkate wa watoto

mkate unamaanisha chakula kwa ujumla

mbwa wadogo

Wayahudi waliona mbwa kuwa ni wanyama najisi. hapa wanamanisha kama sura ya watu wasio Wayahudi

Matthew 15:27

hata hivyo mbwa waadogo hula chkula ... mezani mwa bwana zao

Yule Mwanamke akamjibu Yesu kwa kutumia mazingira yale yale aliyetumia Yesu kwenye mithali. Alimaanisha kuwa wasiokuwa Wayahudi waliweza kupata kiasi kidogo cha kile walichopata Wayahudi amabcho walikuwa wanatupa.

mbwa wadogo

tazama 15"24

na ifanyike kwako kama ulivyotaka

Nitafanya

binti yake alikuwa ameponywa

Yesu alimponya yule binti

wakati huo

ghafla

Matthew 15:29

Maelezo kwa ujumla

Mstari huu unatoa histora ya muujiza amba Yesu anataka kuufanya wakulisha watu elfu nne

viwete, vipofu, bubu vilema na wengine wengi

wale wasioweza kutembea, wale wasioona, wasiongea, na wale ambao miguu yao na mkono haifanyi kazi

waliwaweka katika miguu ya Yesu

waliwaweka katika mbele ya ya Yesu

vilema wakifanywa wazima

vilema wakaw salama

vilema... viwete ... vipofu

watu viwete ... watu vilema ... watu vipofu.

Matthew 15:32

Sentensi unganishi

Hii inaanzisha habari ya Yesu akiwalisha watu elfu nne

wasije wakazimia njiani

"kwa sababu wanaweza kuzimia njiani

ni wapi tunaweza kupata mikate ya kutosha hapa nyikani kushibisha umati huu mkubwa?

hakuna mahali pa karibu tunapoweza kupata mikate ya kutosha huu umati mkubwa

saba na samaki wadogo

mikate saba na samaki wachache wadogo

uketi chini

kaeni mkao wa kula

Matthew 15:36

alitwaa

Yesu alibeba mkononi mwake

akaimega i

akaigawa mikate

na kuwapa

akawapa mikate na samaki

wakakusanya

wanafunzi walikusanya au watu walikusanya

wotewaliokula

watu waliokula

wanaume elfu nne

wanaume 4,000

kwenda sehemu

lile eneo

Magadani

Hili eneo wakati mwingine huitwa Magdala

Matthew 16

Mathayo16 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Mkate

Mkate ni picha maalum katika 16:5-12. Yesu alitumia mjadala wa wanafunzi wake kuhusu mkate ili kuwaonya dhidi ya mafundisho ya Mafarisayo na Masadukayo. Aliyazungumzia mafundisho haya kana kwamba yalikuwa chachu, kiungo ambacho husababisha mkate kuinuka kabla ya kuokwa.

Wakati huo huo, kutajwa kwa mkate katika sura hii ni maana ya kuwakumbusha wasomaji kwamba Yesu alilisha watu elfu tano na mkate (tazama: Mathayo 14:13-21) na pia watu elfu nne (tazama: Mathayo 15:29-39 ). Maana ni kwamba Yesu hutoa mkate mzuri (mafundishoa), lakini Mafarisayo na Masadukayo hawafanyi hivyo.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Mathayo 16:21 huunda mkatizo katika maelezo haya. Katika hatua hii, Mathayo anatoa maoni kuhusu matendo ya Yesu ambayo yataendelea katika siku zijazo. Ni muhimu kwa mtafsiri kuashiria wazi wazi kwamba maoni haya ni kuhusu siku zijazo, yaliyoingizwa katika maelezo.

Paradox

Kitendawili ni taarifa inayoonekana kuwa ya ajabu, ambayo ni kana kwamba inajikana yenyewe, lakini kwa hakika sio ya ajabu. Kitendawili kiko katika sura hii: "Yeyote anayetaka kuokoa maisha yake ataipoteza, na yeyote anayepoteza maisha yake kwa ajili yangu ataipata." (Mathayo 16: 24-28).

<< | >>

Matthew 16:1

Maelezo ya jumla

Hii inaanzisha mapambano kati y a Mafarisayo na Masadukayo

kumjaribu

walimkosoa au walitaka kukamata

ilipokuwa jioni

ni wakati wa siku ambapo juu huzama

hali nzuri ya hewa

hali nzuri, shwali na ya kuvutia

anga jekundu

Wayahudi walijua kuwa, kama anaga litabarika na kuwa jekundu ilikuwa dalili ya kuwa siku inayofuat itakuwa nzuri

Matthew 16:3

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwajibu Mafarisayo na Masadukayo

asubuhi

jua linapochomoza

hali ya hewa mbaya

hali ya mawingu na ya kimbunga

jekundu na mawingu

jekundu na zito

Mnajua kutambua mwonekano wa anaga

mwajua namna ya kutazama na kutambua aina ya hali ya hewa mtakayokuwa nanyo

lakini hamuwezi kutambua ishara za nyakati

lakini hamwezi kutambua kile kinachotokea sasa na kujua maana yake

kizazi kiovu na cha uzinzi

watu amabao si waaminifu kwa Mungu

kinatafuta ishara

tazama 12:38

lakini hakuna ishara yeyote

Mungu hatawapeni ishara

isipokuwa ishara ya Yona

tazama 12:38

Matthew 16:5

Sentensi unganishi

Mandhari yanabadilika nakuto eleka wakati wa mbale. Yesu anatumia nafasi ya kuwaonya wanafunzi juu ya Mafarisayo na Masadukayo

upande wa pili

upande wa pili wa ziwa au upande wa pili wa bahari ya Galilaya

chachu ya Mafarisayo na Masadukayo

Hapa chachu inamaanisha mawazo macahfu na mafundisho yasiyo sahihi ya Mafarisayo Tazama 16:12.

Wakahojiana miongoni mwao

wakajadiliana

eneyi wenye imani ndogo

Ninyi mlio na imani ndogo Tazama 6:30

kwa nini mnawaza... hamkuchukua mikate

Ninasikitika kuwa mnadhani kuwa mlisahau kuchukua mikate kwa sabasbu nimeongea juu ya chahu ya Mafarisayo na Masadukayo.

Matthew 16:9

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwaonya wanafunzi juu ya Mafarisayo na Masadukayo

Je, bado hamtambui na kukumbuka au ... mlivyokusanya

Kwa hakika mnakumbuka ... mlivyokusanya

elfu tano ... elfunne

"5,000 ... 4,000"

au mikate saba ... mlichukua?

kwa hakika mnakumbuka ... mlivyokusanya!

Matthew 16:11

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwaonya wanafunzi wake juu ya Mafarisayo na Masadukayo

Imekuwaje hata hamuelewii kuwa sizungumzi nanyi kuhusu mikate?

"Inatakiwa muelewe kwamba siongei kumaanisha mikate kweli."

chachu ya Mafarisayo n a Masadukayo

tazama 16:12

wao...wao

"wanafunzi"

Matthew 16:13

Sentensi unganishi

Yesu anawauliza wanafunzi kama wanaelewa kuwa yeye ni nani

Lakini ninyi mwasema mimi ni nani?

"Lakini ni ninyi ninaowauliza:mnasema kuwa mimi ni nani?"

wakati

Neno hili limetumika kuonesha mwanzo wa habari kuu au kumtambulisha mtu mwingine, Mathayo anaanza kueleza habari mpya.

Mwana wa Adamu

Yesu anamaanisha yeye mwenyewe

Mungu aliye hai

Hapa neno "hai" linalinganisha Mungu wa Israeli na Miungu wengine wa uongo na masananu ambayo watu waliabudu. Mungu aliye ndiye Mungu pekee mwenye nguvu za kutenda.

Matthew 16:17

Simoni Bar Yona

"Simoni, mwana wa Yona"

damu na nyama havikukufunulia hilo

damu na nyama inamaanisha binadamu

hili kwako

neno "hili" inamaanisha jibu la Petro kwamba Yesu ni Kristo mwana wa Mungu aliye juu

Baba yangu aliye mbinguni

Hicho ni cheo cha muhimu kwa Mungu ambacho kinaelezea uhusiano kati ya Mungu na Yesu

Nami pia ninakwambia

hii inaongeza msisitizo wa kile Yesu alichosema baadaye

wewe ni Petro

jina Petro linamaanisha "mwamba"

juu y a mwamba huu nitalijenga kanisa

hii inamaanisha kuwa Petro atakuwa kiongozi wa jamii ya watu wanomwamini Yesu

Milango ya kuzimu haitalishinda

Maana zinazowezekana:1)"nguvu za kifo hazitaliweza kanaisa au 2) Kanaisa langu zitaivunja nguvu ya kifo kama jeshi liingiavyo katika mji

Matthew 16:19

nitkupa wewe

neno wewe linamaanisha Petro

Funguo za ufalme wa mbinguni

Hapa "funguo" zinamaanisha Yesu akimpatia Petro mamlaka. Hii haimaanishi kuwa Petroni mmliki wa ufalme, lakini ana mamlaka ya kuamu nani ataiingia katika ufalme wa Mungu

ufalme wa mbinguni

Ufalme wa mbinguni limetumika katika Mathayo tu. tumia "mbingu"

fungwa duniani...funguliwa mbinguni

kuwatangazia watu kusamehewa au kuhukumiwa kama ilivyofanyika mbinguni

funguo

kitu kinachotumika kufungua na kufunga milango

chochote utakachokifunga mbinguni ...kifungua duniani kimefungiliwa duniani

Mungu wa mbinguni ataruhusu maombi ya Petro kuruhusu au kufunga duniani

itafunga ... itafunguliwa

Mungu atafunga .. Mungu atafungua

Matthew 16:21

Sentensi unganishi

Yesu antabiri kifochake na anaanza kuwambia wanafunzi wake gharama za kumfuata.

kuanzia muda huo

Baada ya Yesu kuwaamuru wanafunzi wake kutokumwambia yeyote kuwa yeye ni Kristo, alianza kushirikisha kile kitakachotokea Yerusakamu

Kuteswa kwa mambo mengi katika mikono ya wazee na wakuu wa makuhani na waandishi

Hapa "mikono " inamaanisha mamlaka. Ambapo wazee, makuhani na waandishi watamsababishia maumivu

kuuawa

watamuua

jambo hilina liwe mbali n a wewe

"hapana" au "halitatokea" au "Mungu alizuie"

kufufuka siku ya tatu

"siku ya tatu, Mungu atamfanya aishi tena"

rudi nyuma yangu shetani wewe ni kizuizi

Yesu anamaanisha kuwa Petro anafanya kazi kama shatani kwa sababu Petro anajaribu kumzuia Yesu kukamilisha kile ambacho Mungu amemtuma Yesu. "Rudi nyuma yangu kwa sababu unafanya kama shetani! wewe ni kikwazo kwangu.

Matthew 16:24

nifuate

"uwe mwanafunzi wangu" au "uwe mmoja wa wanafunzi wangu"

auchukue msalaba wake na anifuate

msalaba unawakilisha mateso na kifo. lazima anitii hata kiasi cha kufa"

, na kunifuata

"na kunitii"

Kwa yeyote atakaye

"Kwa yeyote anayetaka"

atayapoteza

Hii haimanishi kuwa yule mtu lazima afe. inamaanisha kumwamini Yesu kuwa jambo la muhimu kuliko maisha yake.

kwa ajili yangu

"kwa sababu ananiamini mimi" au " kwa sababu yangu"

atayaokoa

atapata maisha ya kweli

Ni faida gani atakayopata mtu ... akapoteza maisha yake

Haimpi mtu faida ...maisha yake

akaipata dunia yote

hakuna kitu cha thamani duniani kuliko kuishi na Mungu. " kama akipata kila kitu ulimwenguni"

lakini akapoteza maisha yake

"lakini akapoteza maisha yake"

ni kitu gani atakachotoa mtu katika kubadilishana na maisha yake

"Hakuna kitu ambacho mtu atatoa ili kurudisha uhai wake"

Matthew 16:27

Mwana wa Adamu...baba yake

Yesu alikuwa anajirejelea yeye mwenyewe katika nafsi ya tatu kama "Mwana wa mtu"

katika utukufu wa baba yake

"kupata utukufu sawa na Baba yake"

na malaika wake

"na malaika watakuwa pamoja naye" au "na malaika wa Baba watakuwa pamoja na mimi"

baba yake

Hicho ni cheo kikubwa kwa Mungu ambacho kinaelezea uhusiano wa Mungu na Mwana wa mtu, Yesu

kweli nawambia

"Nawaambieni ukweli"

wewe

kiwakilishi cha wingi kinachomaanisha wanafunzi wa Yesu.

hawataonja kifo

"kuonja" inamaanisha kupitia kifo" au "hawatapitia kifo" aua "hawatakufa"

Mpaka watakapomwona Mwana wa Adamu akija katika ufalme wake

"Ufalme" inamaanisha Mwana Adamu akitawala kama mfalme" aua "mpaka watakapomwona wa Adamu akija kutawala kama mfalme"

mpaka watakapomwaona

Yesu bado anaongelea wanafunzi. "mpaka mtakapomwona"

Matthew 17

Mathayo17 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Eliya

Nabii Malaki alitabiri kwamba siku moja Eliya atarudi kabla Masihi hajaja. Yesu anaelezea kwamba Yohana Mbatizaji alitimiza unabii huu kwa kumtumikia Mungu kwa namna ile ile kama Eliya. (Angalia: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#prophet na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#christ)

"Yeye (Yesu) alibadilishwa"

Utukufu wa Mungu unaonekana kama mwanga mkubwa, katika maandiko. Utukufu wa Mungu daima humhofisha mtu anayeuona. Tukio hilo, lililoko katika sura hii, linaitwa "kubadilika," ambako Yesu anabadilika ili aonyeshe utukufu wake wa uungu. (Angalia: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#glory na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#fear)

<< | >>

Matthew 17:1

Maelezo kwa ujumla

Hii inazisha habariya Yesu kubadilika sura

Petro, na Yakobo, na Yohana kaka yake

"Petro, Yakobo, na kaka yake Yakobo Yohana"

Alibadilishwa

"Mungu amembadilisha kabisa Yesu

mavazi

"nguo"

Uso wake ukang'aa kama jua ...kung'aa kama nuru

Hii ni milinganyo inayosisitiza jinsi Yesu alivyong'aa.

Matthew 17:3

Tazama

Neno hili linatutayarisha kuwa tayari kwa taarifa za kushangaza zinazofuata.

kwao

kwa wanafunzi waliokuwa na Yesu amabao ni Petro, Yakobo na Yohana

akajibu na kusema

"sema." Petro hajibu swali.

pamoja naye

"pamoja na Yesu"

ni vizuri kwetu kuwa hapa

Maana zinazowezekana: 1)"ni vizuri kwamba sisi wanafunzi tuko hapa pamoja nawe, Musa, na Eliya au 2)"ni vizuri kuwa wewe, Musa, Eliya, na sisi wanafunzi wote tuko hapa pamoja"

mahala pa kujihifadhi

Maana zinazowezekana: 1)mahali pa watu kuja kuabudia au 2)mahali pa muda pa watu kulala.

Matthew 17:5

Tazama

Hii hutahadharisha msomaji kuwa makini na maelezo ya kushangaza yanayofuata

likawatia kivuli

"lilikuaj juu yao"

ikatokea sauti toka kwenye wingu

"Sauti inamaanisha Mungu aliogea" aua "Mungu aliongea noa kutoka kwenye wingu"

waanafunzi waliposikia

"wanafunzi walimsikia Mungu akiongea"

Walianguka kifulifuli

Wanafunzi waliinama kwa nyuso zao kugusa chini ardhini.

Matthew 17:9

Sentensi unganishi

Tukio lifuatalo lilitokea mara tu baada ya wale wanafunzi watatu kushuhudia Yesu akibadilishwa

Na walipokuwa

Na Yesu na wanafunzi wake

mwana wa Adamu

yeye anajinenea mwenyewe

kwa nini wandishai husema kuwa Eliya atakuja kwanza?

Wanafunzi wanazingatia mafundisho ya kwamba Eliya atarudi kwanza kwa wana wa Israel kabla ya Masihi kurudi

Matthew 17:11

Kurudisha vitu vyote

"kuweka vitu katika mpangilio au utaratibu" au " waandae watu tayari kwa ajili kumpokea Masihi"

Lakini nawaambieni

huu ni msisitizo wa kile Yesu alichosema baadaye

hawa .... yake

Maana zinazowezekana: 1) viongozi wa wayahudi au 2) wayahudi wote

Mwan wa Adamu atakavyoteswa

Hapa "mikono" inamaanisha nguvu. "watamfanya mwana wa Adamu kuteseka"

Mwana wa Adamu

Yesu anajineneea mwenyewe.

Matthew 17:14

Sentensi unganishi

Hii inaanzisha habari ya Yesu akimponya kijana aliyekuwa na roho mchafu.Tukio hili limetokea baada ya Yesu na wanafunzi wake kushuka kutoka mlimani.

umhrumie mwanangu

inamanisha kuwa yule mtu alimtaka Yesu amponye mwanae. "umhurumie mwangu na umponye"

amaekuwa na kifafa

Hii inamaanisha kuwa wakati mwingine hupoteza fahamu

Matthew 17:17

kisichoamini na kilichoharibika

"Kizazi hiki hakimwani Mungu na hakijiui kitu kibaya na kizuri.

nitakaa pamoja nanyi mpaka lini, nitavumiliana nanyi mpaka lini?

nimechoka kukaa pamojana nyi, nichoshwa na kutokuamni kwenu

kijana aliponywa

kijana akawa mzima

tangu saa ile

mara moja

Matthew 17:19

Sisi

waongeaji na si wasikilizaji

Kwa nini tusingeweza kuifukuza?

"Kwa nini tusimfanye pepo amtoke kijana?"

Hakuna kitakachowezekana kwenu kukifanya

"Mtaweza kufanya kitu chochote

kweli nawaambieni

"nawambia ukweli"

kama mtakuwa na imani hata ndogo kama punje ya mbegu haradali

Yesu analinganisha ukubwa wa mbegu ya haradari na kiasi cha imani kinachotakiwa ili kufanya miujiza. inahitajika imani ndogo tu ili kufanya miujiza.

hakutakuwa na kitu chochotte cha kushindikan kwenu

mtaweza kufanya kila kitu

Matthew 17:22

Sentensi unganishi

Yesu anatabiri kifo chake na ufufuo

wamekaa

"wanafunzi na Yesu wamekaa"

Mwan wa Adamu Watamuua

"mmoja atamuua Mwana wa Adamu"

Mwana wa Adamu ...mwa ...watu

inamaanisha yeye yenyewe

Atafufuka

"Mungu atamfufua" au" ataishi tena"

atatiwa

atatolewa

mikononi mwa watu

mikononi inamaanisha mamlaka ya kutwala. "katika utawala wa watu

siku ya tatu

siku ya tau

atafufuka

Mungu atamfufua

Matthew 17:24

Sentensi unganishi

Yesu anamfundisha Petro juu ya kulipa ada ya hekalu

wakati wao

wakati yesu na wanafunzi wake

kodi ya nusu shekeli

kodi juu ya wanaume wote wa kiyahudi ambayo ilitolewa ili kuwezesha kazi za hekaluni

nyumba

mahali Yesu alipokaa

Unafifkiri nini Simoni? wafalme wa dunia ...kutoka kwa wageni?

Yesu anauliza swali hili kumfundisha Simoni asitafute taarifa kutoka kwake. "Sikiliza Simoni, tunafahamu kuwawafalme wa dunia hukusanya kodi kutoka kwa wageni na wala si kwa raia wake.

wafalme wa dunia

viongozi kwa ujumla

Raia

watu chini ya kiongozi au mfalme

wanaotawaliwa

watu walio chini ya mfalme

Matthew 17:26

Sentensi unganishi

Yesu anaendela kumfundisha Petro juu ya kulipa kodi

Maelezo kwa ujumla

Huu ni mwisho wa habariinayoanzi 13:54 amabpo mwandishi amaeelza juu ya upinzani wa wa huduma ya Yesu kuhusu ufalme wa mbinguni

Petro aliposema kutoka kwa wageni

wakati Petro aliposema "ndiyo. hiyo ni sawa ,wafalme hukusanya kodi kutoka kwa wageni"

kutoka kwa wageni

Nyakati hizi za leo. wafalme wanatoza kodi toka kwa raia wake, lakini katika nyakati za zamani wafalme walitoza kodi toka kwa watu waliokuwa wamewashinda na si raia wao.

watawaliwa

Watu chini ya kiongozi au mfalme.

lakini tusije tukawafanya watoza ushuru kutenda dhambi

lakini tusiwafanye watoza ushuru kutenda kuwa na hasira

tupa ndoano

wavuvi hufunga ndoano mwisho wa uzi, na kisha huitupa majini ili kukamata samaki

mdomo wake

"mdomo wa samaki"

shsekeli

sarafu iliyotosha malipo ya kibarau kwa siku moja

chukua

chukua shekeli

kwangu na wewe

wewe inamaanisha Petro. Kila mwanamume alipaswa kulipa shekeli moja. kwa hiyo Shekel moja iliweza kutosha kwa kodi ya Peteo na Yesu

Matthew 18

Mathayo18 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Je, unapaswa kufanya nini "ndugu yako akikukosea"?

Katika sura hii, Yesu anafundisha kwamba ni muhimu kwa wafuasi wake kuacha ugomvi kati yao wenyewe. Anafundisha kwamba kikundi cha waumini lazima kiwe tayari kuwezesha hii kufanyika kwa njia "inayomheshimu Mungu.

Kanisa lina jukuma pia wa kuwahimiza waumini kutubu ikiwa wanafanya dhambi. (Angalia: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#repent na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

<< | >>

Matthew 18:1

Maelezo kwa ujumla

Hii ni mwanzo wa habari mpya inayoanzia 18:34, mahali Yesu anapofundisha juu ya maisha katika uflme wa mbinguni. Hapa Yesu anatumia mtoto mdogo kufundisha wanafunzi wake.

nanai mkuu

Nani ambaye ni wa muhimu zaidi"au "nani kati yetu atakuwa wa muhimu zaid

katika ufalme wa mbinguni

wakati Mungu wetu wa mbinguni atakapoanzisha utawala wake duniani

Kweli nawaambia

"nawambia ukweli" au hii inaongeza msisitizo kwa kile Yesu alichosema baadaye

msipotubu na kuwa ... hamtaweza kuingia

lazima mbadilike .. ili kuingia"

kuwa kama watoto

lazima wawe wanyeyenyekevu kama watoto.

kuingia katika ufalme wa mbinguni

Mungu kutawala kama mfalme

Matthew 18:4

Sentensi unganishi

Yesu anawafundisha wanafunzi wake kwamba wanahitaji kuwa wanyeyekevu kama watoto ili kuwa watu wa muhimu kwenye ufakme wa mbingini

ni mkuu

ni wa muhimu zaidi aua atakuwa ni wa muhimu

katika ufame wa mbinguni

katika ufalme wa mbinguni

kwa jina langu

kwa sababu yangu

anipokea mimi

ni kama ananipokea mimi

Jiwe kuu la kusagia likafungwa shingoni mwake,na kuzamishwa kilindini mwa bahari.

"kama wangemwekea jiwe la kusagia shingoni mwake na kumtupa kilindini mwa bahari"

Jiwe la kusagia

Jiwe kubwa, zito iliyotengenezwa kama duara inayotumika kusagia nafaka kuwa unga .

Matthew 18:7

Sentensi unganishi

Yesu anaendela kutumia watoto wadogo kuwafundisha wanafunzi wake na kuwaonya dhidi ya madhara makubwa ya kuwaangusha watoto

kwa dunia

dunia inamaanisha watu

kwa sababu ya wakati wa kukwazwa

kwa sababu ya mambo yanyowafanya watu kukwazwa

Mkono wako

Yesu anaongea na wanafunzi wake kama ni mtu mmoja.

kwa nyakati hizo huja

kwamba mambo hayo huja yanayowafanya watu kufanya dhambi

kwake kwa mtu yule nyakati hizo

mtu yeyote anayewafnya wengine kufanya dhambi

kama mkon wako ... utupe mbali

Yesu anamaanisha kuwa mtu lazima afanye kila linalolazimika ili kukitoa katika maisha kile kinachomfanya mtu kufanya dhambi

wako ... uki

Yesu anaongea kwa watu wote kwa ujumla

kwenye uzima

uzima wa milele

kuliko kutupwa kwenye moto wa milele ukiwa na mikono yote aua miguu yote

kuliko kuwa na mikono miwil na miguu miwili wakati Mungu anakutupa kwenye moto wa milele.

Matthew 18:9

Ng'oa na tupa

Fungu hili linaonesha ukweli wa kutokuamini na ulazima wa kuizuia kwa gharama yoyote

Ingia uzimani

"Ingia katika uzima wa milele"

Matthew 18:10

Tazameni

Muwe waangalifu

musiwadharau hawa wadogo

"Msidhani kuwa hawa wadogo hawana umuhimu". onyesheni heshima kwa hawa wadogo

kwa maana nawaambia

hii inatia msisitizo kwa kile Yesu alichosema baadaye

mbinguni kuna malaika wao siku zote wakiutazama uso wa baba yangu aliye mbinguni

Yesu anammanisha kuwa malaika wa mbinguni humwambia Mungu juu ya wadogo hawa

Muda wote tazama uso wa

"wapo karibu muda wote"

siku zote wakiutazama uso wa baba yangu

kila mara wako karibu na baba yangu"

baba yangu

Hiki ni cheo muhimu kwa Yesu kinachonesha uhsiano kati ya Yesu na Mungu

Matthew 18:12

Sentensi unganishi

Yesu anaendele kuwatumia watoto wadogo kuwafundisha wanafunzi kueleza ulinzi wa Mungu kwa watu

Unawaza nini?

"Fikiri watu wanavyofanya,"

wewe ... yako

viwakilishi vya wingi

ikiwa mtu ...wasiopotea

Yesu anatumia mfano kuwafundisha wanafunzi

kondoo mia moja ...tisini n a tisa

100 ...99

hatawaacha ...aliyepotea

Yesu anatumia swali kuwafundisha wanafunzi

kweli nawaambia

nawaambia ukweli

Siyo matakwa ya baba yenu wa mbinguni kuwa moja wa wadogo hao apotee

"Baba yenu mbinguni anataka wadogo wote hao waishi"

Matthew 18:15

Sentensi unganishi

Yesu anaanza kuwafundisha wanafunzi wake juuy msamaha

ndugu yao

waumini wenzake

utampata ndugu yako

"mtafanya mahusiano yenu mazuri tena na ndugu yako"

kwa kuwa kwa vinywa vya mashahidi wawili ...kila neno linaweza kuthibitishwa

"mdomo" na "maneno" inamaanisha kile amabcho mtu anasema " ili kwamba wawili au watatu wanaweza kuthibitisha kile unachosema juu ya mwamini mwenzako"

Kwa kuwa kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu kila neno linaweza kuthibitika

Yesu anatumia moja katai ya sheria ambazo Musa alaiwapati watu

Matthew 18:17

akipuuza kuwasikiliza

kama huyo nndugu akipuuza kuwasiliza mashahidiuliokuja nao

kanisani

kwa waumini wote

Mwacheni awe kwenu kama mtu wa mataifa na mkusanya ushuru

"Mchukulie kama utakavyomchukulia mtu wa mataifa au "mtoza ushuru. Maana yake ni kwamba wamwondoe kati ya jamii ya waumini.

Matthew 18:18

mta

viwakilishi vyote hivi viko katka wingi

Funga...fungwa...fungua...funguliwa

tazama 16:19

Itafungwa...itafunguliwa

"Mungu atafunga...Mungu atafungua."

nawaambieni

Msisitizo wa kile Yesu alichosema baadaye

Baba yangu

Hicho ni cheo cha muhimu kwa Mungu kinachoonesha uhusiano wa Mungu na Yesu.

kama wawili wenu

anagalau wawili

wawili au watatu

"wawili au zaidi" au "angalau wawili"

Wamekusanyika

"kutana"

waki ... wao

inamaanisha "wawili wenu"

Baba yangu

Hiki ni cheo muhimu cha Mungu kinachoonesha uhusiano kati ya Mungu na Yesu

Matthew 18:21

Mara saba

"mara 7"

Sabini mara saba

Maana zenye kufaa: 1) "70 mara 7". au 2) "mara 77." kama kutumia namba kutachanganya,unaweza kusema, "mara nyingi kuliko utakavyohesabu"

Matthew 18:23

Sentensi unganishi

Yesu anatumia mfano kufundisha juuya msamaha na mapatano

Ufalme wa mbinguni unafanana

Hii inatoa utangulizi wa mfano. Tazama 13:24

Kusahihisha hesabu na mtumwa wake

"ili awalipe watumwa wake kile walichostahili"

Mtumishi mmoja akaletwa

"mtu fulani akamleta mmoja wa watumishi wa wafalme"

Talanta elfu kumi

"Talanta 10,000" au " fedha nyingi zaidi kuliko mtumishi alizoweza kulipa

Mkuu wake aliamuru auzwe,...na malipo kufanyika

"mfalme aliwaamuru watumishi wake kumuuza huyo mtu...na kulipa deni kwa fedha ya mauzo"

Matthew 18:26

alianguka, akapiga magoti chini

Hii inammanisha kuwa yule mtumwa aliongea na yule mfalme katika hali ua unnyenyekevu mkubwa.

mbele yake

"mbele ya mfalme"

alaisukumwa sana na huruma

"alimhurumia yulemtumwa"

alimwachilia

alimwacha aende"

Matthew 18:28

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwaambia mfano wanafunzi wake

Dinari mia moja

"dinari 100" au "malipo ya kibarua ya siku miamoja"

alimvuta, akamkaba kooni

"yulemtumwa wa kwanza alimkaba mtumwa mwenzake

alimkaba

kumung'ang'nia " au "kamata kwa nguvu"

alianguka

Tazama 18:26

Matthew 18:30

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwaambia mfano wanafunzi wake

alienda na kumtupa gerezani

"yule mtumwa wa kwanza alienda na kumtupa gerezani mtumwa mwenzake"

"watumwa menzake"

"watumwa wengine"

walimwambia bwana wao

"walimwambia mfalme"

Matthew 18:32

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwambia mfano wanafunzi wake

Kisha bwana wa mtumishi yule akamwita

"Kisha mfalme akamwita mtumwa wa kwanza"

ulinisihi

"uliniomba

Je, haukutakiwa kuwa na huruma kwa mtumwa mwenzio?

Mfalme anatuma swalikumkalipia mtumwa wa kwanza. "ulitakiwa ... wewe"

Matthew 18:34

Sentensi unganishi

Yesu anamalizia mfano wake juu ya msamaha na upatanishi

Maelezo kwa ujumla

Huuni mwaisho wa shsemu y a simulizi iliyoanzia 18:1 mahali ambapo Yesu anafundisha juu ya maisha katika ufalme wa mbinguni.

Bwana wake

"Mfalme"

kumkabidhi kwa

"alimtoa kwa" inawezekena kuwa mfalme mwenyewe hakumkabidhi yule mtumwa wa kwanza kwa watesaji," "Aliwaagiza watumwa wake wamkabidhi"

kwa watesaji

"kwa wale ambao wangemtesa"

alichokuwa anadaiwa

Hii inaweza kutafasiriwa kwa mafumo tendaji. Kile ambacho mfalme alimdai yule mtumwa wa kwanza"

baba yangu wa mbinguni

Hiki ni cheo muhimu kwa Mungu kinachoonesha uhusiano kati ya Mungu ya Yesu.

mmoja wenu ... kwenu

Viwakilishi vyote hivi viko katika wingi. Yesu anaongea na wanafunzi wake, lakini mfanohuu unafundisha ukweli ambao unaweza kutumiwa na waamini wote

ndugu yake

"ndugu yake"

moyoni mwenu

Hii ni nahau. "kwa ukweli" au "kwa ukamilifu"

Matthew 19

Mathayo19 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Mafundisho ya Yesu kuhusu talaka

Katika sura hii, Yesu anafundisha kuhusu talaka. Ilikuwa jibu la changamoto lililotolewa na Mafarisayo. Mafundisho yake Yesu yanategemea nia ya awali ya Mungu katika kuunda ndoa. Yesu anaonyesha makosa ambayo viongozi wa dini walifanya katika desturi zao kuhusu ndoa.

<< | >>

Matthew 19:1

Maelezo kwa ujumla

Huu ni mwanzo wa simulizi jipyaamabalo linanaishia 22:45, ambayo inaonesha Yesu akihudumia huko Yudea

Maelezo kwa ujumla

Mistari hii inatoa historia ya jinsi Yesu alivyokuja Yudea

Ilitokea wakati

Habari inaeleza jinsi Yesu alivyositisha mafundisho yake kwenda tukio lililofuata

Alipomaliza maneno hayo

kile Yesu alichofundisha kuanzi 18:1

akaondoka

"alitembea kutoka" au "akatoka"

Matthew 19:3

Sentensi unganishi

Yesu anaanza kufundisha juu ya ndoa na talaka

wakamjia

"walikuja kwa Yesu

wakaimjaribi wakisema

kujaribu limetumika kwa maana hasi. "wakamkosoa kwa kumuuliza" au "walitaka kumkamata kwa kumuuliza"

Hamkusoma kwamba yeye aliyewaumba mwanzo aliwauumba mume na mke?

Yesu anatumia swali kuwajibu Mafarisayo. "Kwa hakika mmesoma kwamba mwanzo Mungu aliwaumba watu,aliwaumba"mume na mke

Matthew 19:5

Maelezo kwa ujumla

Katika mstari wa 5, Yesu ananukuu kutoka Mwanzo kuonesha kuwa Mume na mke hawatakiwi kuachana

Na yeyealiyewaumba pia alisema, 'kwa sababu hii ...mwili mmoja?

Huu ni mwandelezo wa swali ambal oYesu alilitumia kuwaliza Mafarisayo katika 19:3. Hii nukuu ya moja kwa moja inaweza kuelezwa kama nukuu isyo ya moja kwa moja. Kwa hakika mnajua kuwa Mungu alisema kuwa kwa sababu hii...mwili mmoja.

kwa sababu hii

sababu ya mwanamume kumwacha baba na mama ni kwamba Mungu alimuumba mwanamke kuwa msaidizi wa mwanamume

Ungana na mke wake

"Kaa na mke wake"

Na wale wawili watakuwa mwili mmoja

"watakuwa kama mwili mmoja"

Hivyo si wawili tena, bali mwili mmoja

Kwahiyo mwanamume na mwanake siwawil tena bali mwili mmoja"

Matthew 19:7

Wakamwambia

"Mafarisayo walimwambia Yesu"

Tuamuru

"Amuru sisi Wayahudi"

Hati ya talaka

Waraka unaohalalisha kisheria mwisho wa ndoa

kwa sabau ya ugumu wa mioyo yenu

kwa sababu ninyi ni wasumbufu

kwa ugumu ... aliwaruhusu ....wake zenu

wewe na yenu ziko katika wingi. Yesu anaongea na Mafarisayo, lakini Musa aliwapa shaeria hii miaka mingi iliyopita kwa mababu zao. amri ya Musa ilitumika kwa Wayahudi wote.

tangu mwanzo

"Wakati Mungu alipomuumba mume mke hakupanga waachane"

nawaambieni

anaongeza msisitizo

na kumwoa mwingine

na kumwoa mwanamke mwingine

Na mwanaume anayemwoa mwanamke ambaye ameachwa amefanya uzinzi

Maandishi mengi ya mwanzo hayajumuishi maneno haya.

Matthew 19:10

walioruhusiwa

wale ambao Mungu amewaruhusu au ambao Mungu huwaruhusu

kwa kuwa wapo matowashi waliozaliwa tokea tumboni mwa mama

kwa kuwa kuna wanaume waliozaliwa kuwa matowashi

Matowashi waliojifanya matowashi

kuna matowashi waliofanywa kuwa matowashi

kuna matowashi waliojifanya kuwa matowashi

inawweza kumaanisha 1)wanaume waliojifanya wenyewe kwa kutoa sehehmu zao za siri 2) wanaume waliochagua kutokuoana ni wasafi katika swala la zinaa.

kwa ajili ya ufalme wa mbinguni

ualame wa mbinguni inamaanisha Mungu kutawala kama mfalme

Pokea mafundisho haya...pokea

Anayeweza kupokea mafundisho haya na ayapokee."

Matthew 19:13

Sentensi unganishi

Yesu anawapokea na kuwabariki wat.oto wadogo

Kisha akaletewa baadhi ya watoto wadogo

watu baadhi wakaleta watoto wadogo kwa Yesu

Kibali

"Ruhusu"

Msiwazuie kuja kwangu

Msiwazuie kwa kuja kwangu

Kwa maana ufalme wa mbinguni ni wa watu kama hao

Mungu kuwa mfalme kwa watu anaowatawla

ni wa watu kama hao

ni wa watu kama watoto

Matthew 19:16

Sentensi unganishi

Yesu anaongelea habariya mtu tajiri na jinsi iwezavyo kumgharimuamafuatapo Yesu

Tazama

Mwandishi anamweka mtu mpya kwenye habari.Lugha yako inaweza kuwa na njia nyingine ya kufanya hivyo.

Kitu kizuri

kitu kinachompendeza Mungu

kwa nini unaniuliza ni kitu gani kizuri

usiniulize juu ya kitu kilicho kizuri

kuna mmoja tu aliye mwema

"Mungu pekee ndiye mwema aliyekamilka"

kuingia uzimani

"ikupokea uzima wa milele"

Matthew 19:18

mpende jirani yako

Wayahudi waliamni kuwa majirani zao ni wayahudi tu. Yesu alipanua maana ya jirani il kujuisha watu wote.

Matthew 19:20

kama ukitaka

"kama unataka"

uwape masikini

kwa wale amabao ni masikini

utakuwa na hazina mbinguni

Mungu atakuzawadia mbinguni

Matthew 19:23

Sentensi unganishi

Yesuanawaeleza wanafunziwake zawadi ya kutokutafuta mali ya hapa duniani na uhusianao wa kumfuata yeye.

kweli nawaambia

nawaambia ukeli. huunimsisitizo wa kile Yesu alichosema baadaye

kuingia katika ufalme wa mbinguni

kumpokea Mungu wa mbinguni kama mfalme wetu.

ni rahisi ... ufalme wa mbinguni

Yesu anatumia mbalagha kusisitiza kuwa ni vigumu kwa tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.

Tundu la sindano

Tobo katika mwisho wa sindano kwa kupitishia uzi

Matthew 19:25

Wakashangaa sana

"wanafunzi wameshtushwa au kushangazwa." walishangazwa kwa sababu waliamini kuwa na utajiri ilikuwa ishara ya kukubarika kwa Mungu

Ni nani basi atakayeokoka?

Kwa hiyo hakuna ambayae Mungu atamwokoa" au "hakuna ambaye atapokea uzima wa milele

Tumeacha kila kitu

"tumeacha utajiri wetu wote" au "tumeacha miliki yetu yote"

Hivyo tutapata nini?

"Kitu gani kizuri Mungu atakachotupa?"

Matthew 19:28

kweli nawaambia

msisistizo wa kile kinachofuatia

kaika uzao mpya

"wakatimpya" inamaanisha wakatiMungu akirudisha kila ktu" au "wakati ule ambao Mungu atafanya kila kitu kuwa kipya.

Mwana wa Adamu

Yesuanaonge juuyake mwenyewe

atakapoketikatika kiti cha enzi

Kukaa katika enzi kunamaanisha kutawala kama mfalme. enzi yake kuwa tukufu minawakilisha "utawala wake kuwa wa utukufu" au "kutawala kwa utukufu kama mfalme"

mtaketi juu ya viti kumi na viwili vya enzi

Hapa "enzi" inamaanisha kutawala kama mfalme. Wanafunzi hawatakuwa sawa na Yesu ambaye pia yuko kwenye enzi.. Watapokeamamlaka kutoka kwake."kukaa kama kwenye enzi 12"

makabila kumi na mawili ya Israel

Hapa "makabila" inamaanisha wtu kutoka kabila hizo

Matthew 19:29

kwa ajili ya jina langu

hapa "jina" linamaanisha nafasi nzima. "kwa sababu yangu" au " kwa sababu ananiamini mimi"

atapata mara mia

Kupokea kutoka kwa Mungu mara 100 na vitu vingine vizuri kama walivyoacha

kuurithi uzima wa milelel

Hii ni nahau inayomaanisha "Mungu atawabariki na uzima wa milele" au "Mungu atawafanya kuishi milele

Lakini wengi walio wa kwanza sasa, watakuwa wa mwisho, na walio wa mwisho watakuwawa kwanza.

Yesu analinganisha kizazi hiki na kile kijacho. Wale ambao ni wa muhimu sasa Mungu atawafanya kuwa si wa muhimu atakapoanzisha utawala wake hapa duniani. Wale wanaoonekana si wa muhimu leo Mungu atawafanya kuwa wa muhimu atakapoanzisha utawala wake.

Matthew 20

athayo 20 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Mfano wa mwenye shamba na shamba lake la mizabibu

Yesu anatumia mfano huu (Mathayo 20:1-16) ili kuwafundisha wanafunzi wake kwamba kanuni za Mungu kuhusu kile kilicho sawa ni tofauti na kanuni za binadamu.

<< | >>

Matthew 20:1

Sentensi unganishi

Yesu anaelzea mfano wa mtu mmoja aliyekuwa anamiliki shamba anayeajiri wafanya kazi, ili kufafanua jinsi atakavyowalipa watu wa ualme wake.

Kwa maana ufalme wa mbinguni unafanana

Tazama 13:24

Baada ya kukubaliana

"baada ya mmiliki wa shamba kukubaliana"

Dinari moja

"malipo ya kibarau ya siku moja"

aliwatuma kwenda katika shamba lake la mizabibu

aliwatuma kwenda kufanya kazi katika shamba lake

Matthew 20:3

Sentensi unganishi

Yesu anaendela kuelza mfano

Alienda tena

"Mmiliki wa shamba alienda tena"

baada ya masaa matatu

saa ya tatu ni sawa na saa tatu asubuhi

wamesimama bila kazi katika eneo la soko

"Wamesisma eneo la soko pasipo kufanya kazi yeyote"

eneo la soko

Hili ni eneokubwa la wazi ambapowatu huuza na kununua chakula na bidhaa zingine.

Matthew 20:5

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kusimulia mfano

akaenda tena

"Mmiliki wa shamba akaenda tena"

saa ya sita

saa ya sita ni sawa na sasa sita mchana. saa ya tisa ni sawa na saa tisa mchana

alifanya hivyo hivyo

Hii inamaanisha yule mmilikiwashamba alienda sokono kuaajiri atu wengine

saa ya kumi n a moja

Hii ni sawa na saa kumi na moja mchana

bila kazi

"bila kufanya chochote" au "bila kuwa na kazi yote"

Matthew 20:8

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kueleza mfano

kwa kuanza na wa mwisho hadi wa kwanza

Waweza kuzi kuyafanya maelezo h aya yaeleweke kwa uwazi. "Kwa kuanza na wafanyakazi niliowaajiri mwishoni, kisha lipa wafanyakazi niliowaajiri kwanza"

walioajiriwa

Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji. "wale aliowaajiri mwenye shamba"

Dinari moja

"malipo kibarua ya siku moja"

Matthew 20:11

Sentensi ungsnishi

Yesu anaendelea kueleza mfano

Baada ya kupokea

"pindi wafanyakazi waliofanya kazi kwa muda mrefu walipopokea"

Mmiliki wa shamba

"mmiliki shamba" au "mwenye mizabibu"

umewalinganisha na sisi

"umewalipa kiasi kilekile cha fedha sawa na ulivyotulipa"

Sisi tumebeba mzigo kwa siku nzima na kuungua na joto

Kirai "tumebeba mzigo kwa siku nzima" ni nahau inayomaanisha kuwa "sisi ambao tumefanya kazi kwa siku nzima tukiungua na joto la jua"

Matthew 20:13

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kueleza mfano

Mmoja wao

"mmoja wa wafanyakazi waliofanyakazi kwa muda mrefu

Rafiki

Tumia neno ambalo mtu moja angelitumia kumtambulisha mtu mwingine ambaye anamkemea kwa upole

Je, hatukukubaliana na mimi kwa dinari moja

Mmilki wa shamba anatumia swali kumkemea mfanykazi aliyekuwa akilalamika. "tumeshakubaliana kuwa nitakulipa dinari moja"

Dinari moja

"malipo ya kibarua ya siku moja"

Matthew 20:15

Sentensi unganishi

Yesu anahitimisha mfano wake juu ya mmiliki wa shamba aliyeajili wafanya kazi

Je! si haki kwangu kufanya kile ninachotaka juu ya mali zangu?

Yule mmiliki wa shamba anatumia swali kuwanyamazi wafanyakazi waliokuwa wakilalamika. "Ninaweza kufanya chochote ninachotakajuuya mali yangu"

Au jicho lako ni ovu kwa sababu mimi ni mwema?

Yule mmiliki wa shanba anaatumia swali kuwanyamazisha wale wafanyakazi waliokuwa wakilalamika. "Msiwe na wivu kwa sababu ya ukarimu wangu kwa watu wengine

Au mnaona wivu kwa sababu ya ukarimu wangu?

Yule mmiliki w a shamba anatumia swali kuwanyamazisha wafanyakazi waliokuwa wakilalamika. "Msione wivu kwa sababu ya ukarimu kwa watu wengine"

wa mwisho atakuwa wa kwanza na kwanza atakuwa wa mwisho.

Tazama 19:29

Hivyo wa mwisho atakuwa wa kwanza

Yesu anasema kwa kuhitimisha kwa mfano huu. "Ndipo Yesu aliposema. 'wa mwisho atakuwa wa kwanza'"

Matthew 20:17

Sentensi unganishi

Yesu anatabiri juu ya kifo na ufufuo wake kwa mara ya tatu wakati akisafiri na wanafunzi wake

alipokuwa akipanda kwenda Yerusalemu

Yesu alikuwa juu ya mlima kwa hiyo watu walipanda kwenda pale.

Tazama tunaelekea

Yesu anatumia neno "tazama" ili kuwajengea usikivu wanafunzi wake juu kile anachotaka kuwaambia.

tunaelekea

Kiwakilishi "tu" kinamaanisha Yesu na wanafunzi wake.

Mwana wa Adamu atatiwa

Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji "mtu fulani atamtoa Mwana wa Adamu"

mwana wa Adamu ... watamhumkumu ... ata

Yesu anaongea juu yake akitumia nafsi ya tatu. Kama inawezekana unaweza kutafsiri hii kwa kutumia nafsi ya kwanza

Watamtoa.. ili kumdhihaki

Makuhani wakuu na waandishi watamhukumu na kumtoa kwa watu wa mataifa, na watu wa mataifa watamdhihaki.

kumchapa

"kumchapa" au "kumpiga kwa mijeredi"

siku ya tatu

siku ya 3

atafufuka

Hi inaweza kuelezwa kwa mfumo tendaji. "Mungu atamfufua"

Matthew 20:20

Sentensi ungsnishi

Akijibu swali ambalo Yesu aliulizwa na mama wa wale wanafunzi wawili, Yesu anafundisha wanafunzi wake juu ya mamlaka na kuwatumikia wengine katika ufalme wa mbinguni

Wana wa Zebedayo

Hii inamaanisha Yakobo na Yohana

mkono wako wa kulia ... mkono wako wa kushoto

Maana yake ni uwezo wa kuwa na nguvu, mamlaka, na heshima.

katika ufalme wako

Hapa "ufalme inamaanisha utawala wa Yesu kama mfalme. "utakapokuwa mfalme"

Matthew 20:22

Haujui

Hapa "ham" iko katika wingi na inamaanisha mama na watoto

Je! unaweza

Hapa "mna" ni wingi, lakini Yesu anasema na wale wana wawili.

kukinywea kikombe ambacho nitakinywea

Hii ni nahau inayomaanisha kupita katika mateso. "kupitia mateso ambayo punde nitayapitia"

wakamwambia

"wale wana wa Zebebdayo walimwambia" au "Yakobo na Yohana walisema"

kikombe changu hakika mtakinywea

Hii ni nahau kupitia dhiki. "kwa hakika mtateseka kama nitakavyoteseka

mkono wa kulia ... mkono wa kushoto

tazama 20:20

ni kwale ambao imekwisha kuandaliwa na baba yangu

Hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji. "Baba yangu amekwisha kuyaandaa hayo maeneo, na atawapatia wale anaowachagua.

Baba yangu

Hiki ni cheo muhimu kwa ajili ya Mungu kinachoonesha mahusiano kati ya Yesu na Mungu.

waliposikia hivyo

"Waliposikia ambacho Yakobo na Yohana walimwuliza Yesu"

walihuzunishwa sana na wale ndugu wawili

Kama inawezekana unaweza kukiweka wazi kilichowahuzunisha wale wanafunzi kumi. "Walikasirishwa sana na wale ndugu wawili kwa sababu kilammoja wao alitaka kuketi kwenye upande wa heshima karibu na Yesu.

Matthew 20:25

Sentensi unganishi

Yesu anamalizia kufundisha juu ya mamlaka na kuwatumikia wengine

aliwaita

"aliwaita wale thenashara"

watawala wa wa mataifa huwatiisha,

watawala wa mataifa hulazimisha watu wa mataifa kufanya kile watawala wanataka.

watawala wa mataifa

"watawala wa watu wa mataifa"

huwatiisha

"huwatawalawatu"

yeyote atakayetaka

"yeyote atakaye" au "yeyote atamaniye"

kuwa wa kwanza

"kuwa wa muhimu"

Mwana wa Adamu ... maisha yake

Yesu anaonge juu yake mwenyewe kwa kutumia nafsi ya tatu. kama inawezekana unaweza kuitafsiri hii katika nafsi ya kwanza.

hakuja kutumikiwa

Hii inaweza kutafsiriwa katika mfumo tendaji. "Hakuja ili kwamba watu wengine wamtumikie" au "sikuja ili kwamba watu wengine wanitumikie"

bali kutumika

"bali kuwatumikia watu wengiine"

na kutoa uhai wake

Hii ni nahau. "kufa"

kuwa ukombozi kwa wengi

Neno "ukombozi" htumika kwa maana ya kuwafanya wengine kuwa huru kutoka gerezani au utumwani. Hii ni sitiari ya Yesu kuwaokoa watu kutoka kwenye hukumu ya adhbu ya Mungu kwa ajili y a dhanbi zao

kwa wengi

"kwa ajili ya watu wengi"

Matthew 20:29

Sentensi unganishi

Hii inaanza na habari ya Yesu akiwaponya vipofu wawili

Wakati wakitoka

Hii inaongelea wanafunzi na Yesu

ulimfuata

"ulimfuata Yesu"

vipofu wawili wameketi

Wakati mwingine jambo hili limetafsiriwa kama "Tazama kulikuwa na wanaume wawili weameketi." Mwandishi anatambulisha watu wawili kwenye hii habari. Lugha yako inaweza kuwa na namna ya kulifanya jambo hili.

waliposikia

"wale vipofu wawili waliposikia"

na waliona

wakati mwingine hutafsiriwa , "Tazama" Mwandishi anamwambia msomaji kuwa makini kwa maelezo ya kushangaza yanayofuata. Lugha yako inaweza ikawa na njia fulani ya kufanya hivi.

Alikuwa akipita

Alikuwa akitembea kati yao

Mwana wa Daudi

Yesu hakuwa mwana halisi wa Daudi, Kwa hiyoinaweza kutafsiriwa kama "kizazi cha mfalme wa Daudi." Hata hivyo "mwana wa Daudi " ni cheo cha Masihi, na huenda wale wanaume walikuwa wakimwita Yesu kwa cheo hiki.

Matthew 20:32

Aliwaita

Aliwaita vipofu

je! mnatamani?

"je! mnataka"

kwamba macho yetu yafumbuliwe

Kirai cha "macho yetu yafumbuliwe" ni nahau inayomaanisha kuweza kuona tena. "tunataka utufanye kuona" au "tunataka uwezo wa kuona"

akiwa amevutwa na huruma

"kuwa na hurma" au "kusukumwa na huruma kwa ajili yao"

Matthew 21

Mathayo 21 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri hupendelea kuweka kando kidogo nukuu za Agano la Kale. ULB na tafsiri nyingine nyingi za Kiingereza huingiza mistari yote ya 21:5,16 na 42, ambayo ni nukuu kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

Hosana

Hili ndilo neno ambalo watu walisema wakipiga kelele walipomkaribisha Yesu huko Yerusalemu. Ilikuwa ni tamko la sifa, ingawa pia ilikuwa neno la Kiebrania linalomaanisha, "Tuokoe!"

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Ufalme wa Mungu utaondolewa kutoka kwenu"

Wasomi wametofautiana kuhusu maana ya maneno haya. Swali muhimu ni hili: Je, tukio hili itakuwa la kudumu au la muda? Ikiwezekana, uziache wezekano zote mbili kuwa wazi katika tafsiri yako.

<< | >>

Matthew 21:1

Sentensi unganishi

Hii inaanzisha habari ya Yesu akiingia Yerusalemu. Yesu anawapa maalekezo ya kile wanachopaswa kufanya.

Bethfage

Hikini kijiji kilichoko karibu na Yerusalemu

mwanapunda amefungwa

"mwanapunda ambaye amefungwa na mtu"

amefungwa pale

"amefungwa kwenye nguzo" au "amefungwa kwenye mti.

Matthew 21:4

Taarifa kwa ujumla

Hapa mwandishi anamnukuu nabii Zecharia kuonesha kuwa Yesu anataimiza unabii kwa kumpanda mwanapunda kuelekea Yerusalemu.

Sasa

Hili neno limetumika hapa kuonesha mwanzo wa habari mpya. Hapa Mathayo anafafanua jinsi matendo ya Yesu yanatimiza maandiko

Jambo hili lilitokea lile lililonenwa ili kupitia kwa nabii litimizwe

Jambo hili linaweza kutafsiriwa katika mfumo tendaji. "Hili lilitokea ili Yesu atimize kile alichosema Mungu kupitia manabii tangu zamani za kale"

kupitia kwa nabii

"kupitia kwa nabii Zekaria"

Binti wa sayuni

Binti wa mji inamaanisha watu wa ule mji. "watu wa mji ule" au"watu waishio Sayuni"

Sayuni

Hili ni jina jingiine la Yerusalemu

Mwanapunda mme, mwanapunda mchanga

Neno mwanapunda na mwanapunda mchanga inamaanisha mnyama yuleyule, haimaanishi wanyama wawili tofauti

mwanapunda

dume changa la punda

Matthew 21:6

Mavazi

Makutano wakatandaka mavazi yao chini, na wengine wakakata matawi ya miti wakayatandika barabarani

Matthew 21:9

Hosana

Neno la Kiebrania linalomaanisha "Tuokoe" lakini pia linaweza kumaanisha "Kumsifu Mungu!"

Mwana wa Daudi

Yesu hakuwa mwana halisi wa Daudi, kwa hiyo hii inaweza kutafsiriwa kama "kizazi cha mfalme Daudi. Lakini pia, "Mwana wa Daudi" ni cheo cha Masihi, Huenda makutano walikuwa wakimwita Yesu kwa cheo hiki.

kwa jina la Bwana

Hapa "kwa jina la Bwana" inamaanisha "kwa nguvu ya Bwana" au "kama mwakilish wa Bwana"

Hosana juu zaidi

Neno "juu zaidi" linamaanisha Mungu atawalaye kutoka juu mbinguni. "Mungu asifiwe, ambaye yuko juu mbinguni" au "Sifa kwake Mungu"

Mji mzima ulitaharuki

Neno "mji" linamaanisha wakazi wa mji huo. "Watu wengi mjini kote walitaharuki"

Matthew 21:12

Sentensi unganishi

Hii inaanzisha habari ya Yesu alipoingia Hekaluni

Maelezo kwa ujumla

Katika msari wa 13, Yesu anamnukuu nabii Isaya kuwakememea wachuuzina wabadilishaji wa fedha.

Yesu akaingia hekaluni

Yesu hakuliingia lile hekalu halisi. Aliingia kwenye lile korido la hekalu

waliokuwa wakinunua na kuuza

Wachhuzi waliokuwa wakiuza wanyama na bidhaa ziingine ambavyo wasafiri walinunua ili wapate sadaka halisi ya kutoa hekeluni.

Akawaambia

"Yesu aliwaambia wale waliokuwa wanabadilisha fedha na kununua na kuuza vitu"

Imeandkikwa

Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji. "Nabii aliandika zamani za kale" au "Mungu alishasema tangu zamani

Nyunba yangu itaitwa

"Nyumba yangu itaitwa"

Nyumba yangu

Kiwakilishi "yangu" kinamaanisha Mungu "Nyumba" inamaanisha hekalu

nyumba ya maombi

"mahali ambapo watu wataomba

Pango la wanyang'anyi

Yesu anatumia sitiari kuwakemea watu wanouza na kununua bidhaa hekaluni. "Kama mahali ambapo wanyang'nyi hujificha"

vipofu na vilema

wale waliokuwa vipofu na vilema"

mlemavu

kuwa na mguu ulioumia ambao unaosababisha kutembea kwa tabu"

Matthew 21:15

Maelezo kwa ujumla

Katika mstari wa 16,Yesu anatumia nukuu toka Zaburi kuthibitisha jinsi watu walivyokuwa wamemwitikia

maajabu aliyoyataenda

"vitu vya kushangaza" au "miujiza." Hii inamaanisha Yesu alivyowaponya vipofu na vilema kati ka 21:12

Hosana

Tazama 21:9

Mwana wa Daudi

Tazama 21:9

walishikwa na hasira

Inamaanisha kuwa walishikwa na hasira kwa sababu hawakuamini kuwa Yesu ndiyo Kristo na hawakutaka watu wamsifu. "Walikasirika sana kwa sababu watu walikuwa wanamsifu"

umesikia kile kinachosemwa na hawa watu?

Wakuu wa Makuhani na waandishi wanauliza swali hili kumkemea Yesu kwa sababu wanamchukia, "Usiwaruhusu watu kusema mambo haya juu yako"

Lakini hamjawahi kusoma ... sifakamili?

Yesu anauliza swali hili kuwakumbusha wakuu wa makuhani na waandishi kile walichosoma kwenye maandiko. "Naam, nawasikia, lakini inawapasa mkumbuke mlichokisoma katika maandiko ... sifa"

Lakini hamkusoma...sifu'?

"Ndiyo nimewasikia lakini mnatakiwa kukumbuka mlichokisoma katika maandiko matakatifu...sifu'."

kutoka kwa midomo ya watoto na watoto wachanga mnayo sifa kamili

Kirai hiki "kutoka kwenye midomo" kinamaanisha kuongea. "uliwafanya watoto na watoto wachanga kusema sifa kamili"

Yesu akawaacha

"Yesu aliwaacha makuhani wakuu na waandishi"

Matthew 21:18

Sentensi unganishi

Yesu anatumia mtini kuwafundisha wanafunzi juu ya imani na maombi

Sasa

Hili neno limetumika kuonesha mwanzo wa habari mpya. Mathayo anaeleza kuwa Yesu alikuwa na njaa na ndiyo sababu anasimama kwenye ule mtini.

ukanyauka

"ukafa"

Matthew 21:20

Imekuwaje mtini umenyauka mara moja?

Wanafunzi wanatumia swali kuonesha mshangao wao. "Tumeduwaa kuona kuwa ule mtiini umenyauka haraka!"

kweli nawaambieni.

"Nawaambia ukweli." Kirai hiki kinaonggeza msisitizo wa kile Yesu anachosema baadaye.

kama mkiwa na imani na bila wasiwasi

kama mtaamini kwa ukweli

kunyauka

"kukauka na kufa"

mtauambia hata huo mlima, 'uchukuliwe na kutupwa baharini;

mtaweza kuumbia mlima huu kuondoka na kutupwa baharini"

itafanyika

itatokea

Matthew 21:23

Sentensi unganishi

Hii inaanzisha habari ya viongozi wa dini wakimhoji Yesu

alipofika hekaluni

Inamaanisha kuwa Yesu hakuingia hekaluni ndani. Aliingia kwenye korido la hekalu

mambo haya

Hii inamaanisha mafundisho na uponyaji wa Yesu mle hekaluni. Pia inaweza kumaanisha tukio lililofanyika siku moja kabla la Yesu kuwafukuza wanunuzi na wachuuzi.

Matthew 21:25

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwajibu viongozi wa dini

ulitoka wapi

"alipata mamlaka toka wapi?"

tukisema, ulitoka mbinguni; atatuambia, kwa nini hamkumwamini?

"kama tukisema kuwa tunaamini kuwa Yohana alipokea mamlaka toka mbinguni, Yesu atatuuliza kuwa kwa nini hatukumwamini Yohana"

Toka mbinguni

"mbinguni" inamaanisha Mungu."Kutoka kwa Mungu mbinguni"

Kwa nini hamkumwamini?

Basi mngekuwa mmemwamini Yohana Mbatizaji"

lakini tukisema, 'ulitoka kwa watu'

"lakini kama tukisema kuwa tunaamini kuwa Yohana alipokea mamlaka kutoka kwa watu"

tunawaogopa watu

tunaogopa kile makutano watakachotufikiria au kile watakachotufanyia"

Wote wanamwona Yohana kama nabii

"Wanaamini kuwaYohana ni nabii"

Matthew 21:28

Sentensi unganishi

Yesu anatumia mfano wa wana wawili kuwakemea viongozi wa dini na kufafanua kutokuamini kwao

Lakini mnafikiri nini?

Yesu anatumia swali ili kuwafanya viongozi wa dini wafikirie zaidi juu ya mfano aliotaka kuwaambia. "Niambieni mnafikiri nini juu ya kile ninachotaka kuwaambia"

akabadilisha mawazo yake

Hii inamlenga yule mwana akifikiri kana kwamba alikuwa na fikra zaidi ili achague

Matthew 21:31

Wakasema

"Makuhani wakuu na wazee walisema"

Yesu akawaambia

Yesu aliwaambia wakuu wa makuhani na wazee"

Kweli nawaambieni

"Nawaambia ukweli." Kirai hiki kinaongeza msisitizo wa kile ambacho Yesu atasema baadaye

Wakusanya ushuru na makahaba wataingia kwenye ufalme wa Mungu kabla Yenu kuingia

Neno "ufalme wa Mungu" linamaanisha utawala wa Mungu kama Mfalme. "Mungu atakaposimamisha utawalawake duniani, atawabariki watoza ushuru na makahaba kwa kuwatawala kabla ya kufanya hivyo kwenu"

kabla yenu kuingia

Yaweza 1)Yesu atawapokea watoza ushuru na makahaba kabla ya kuwapokea viongozi wa dini 2) Mungu atawapokea watoza ushuru na makahaba badala ya kuwapokea viongozi wa dini wa Kiyahudi

Yohana alikuja kwenu

Kiwakilishi cha "ninyi" ni cha wingi na kinamaanisha watu wote wa Israel na wala si viongozi wadini tu. "Yohana alikuja kwa watu wa Israel"

kwa njia iliyo nyoofu

Hii ni nahau inayomaanisha kuwa Yohana aliwaonesha watu njia sahihi ya maisha. "na aliwaambia njia sahihi ambayo Mungu anataka ninyi muishi"

hamkumwamini

kiwakilishi cha"hamku.." ni cha wingi. nacho kinamaanisha viongoziwa dini.

Matthew 21:33

Sentensi unganishi

Kuwakemea viongoziwa dini na kufafanua kutokuamini kwao, Yesu anaeleza mfano wa watumishi wapinzani.

Mtu mwenye eneo kubwa la aridhi

"mtu anayemiliki sehemu ya mali"

uzio

"ukuta" au "kizuizi"

akachimba shinikizo

"alichimba shimo la kukamulia zabibu"

akalikodisha kwa watunza zabibu

"kuwaweka wakulima wa mizabibu kuwa wasimamizi wa shamba la mizabibu" Mwenye shamba bado ni mmliki wa shamba.

Wakulima wa mizabibu

watu waliojua jinsi ya kutunza mizabibu na divai

Matthew 21:35

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuelezea mfano

Watumishi wake

Watumwa wa "Mtu mwenye shamba kubwa"

Matthew 21:38

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuelezea mfano.

Matthew 21:40

Sasa

Neno "sasa" halimaanisha "wakati huu," bali limetumika kuvuta usikivu kwa ajili ya fundisho linalofuata.

Wakamwambia

"Watu wakamwambia Yesu"

Matthew 21:42

Sentensi unganishi

Yesu anaanza kuelezea mafano wa watumishi wapinazani

Maelezo kwa ujumla

Yesu anamnukuu nabii Isaya kuonesha kwamba Mungu atamheshimu yule ambaye viongozi wa dini wanamkataa.

Yesu akawaambia

Tazama 21:40

Hamkusomakatika maandiko ... machoni'?

"Fikiria juu ya kile ambacho mmesoma ... macho"

Jiwe waliliolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la pembeni

Yesu ananukuu kutoka Zaburi. Hii ni sitiari inamaanisha viongozi wa dini, kama wajenzi, watamkataa Yesu, lakini Mungu atamfanya kuwa wa muhinmu katika ufalme wake, kama jiwe kuu la pembeni katika ujenzi.

limekuwa jiwe kuu la pembeni

"limekuwa jiwe kuu la pembeni"

Hili lilitoka kwa Bwana

"Bwana ndiye aliyefanya haya mabadiliko

inashangaza machoni petu

Kirai cha "machoni petu" kinamaanisha kuona. "ni maajabu kuona"

Matthew 21:43

Nawaambieni

Hii inaongeza msisitizo juu ya kile ambacho Yesu anasema baadaye

wa..

Kiwakilishi cha wa... ni cha wingi. Yesu alikuwa anaongea na viongozi wa dini na Wayahudi pia katika ujumla wao.

Ufalme wa Mungu utatwaliwa kutoka kwenu na kupewa taifa linalojali matunda yake

Neno "ufalme wa Mungu" inamaanisha utawala wa Mungu kama mfalme. "Mungu atawakataa, Wayahudi, na atakuwa mfalme wa watu toka mataifa mengine watakaozaa matunda"

linalojali matunda yake

Hii ni nahau inayomaanisha utii. "wale wanaotii amri za Mungu"

Yeyote atakayeanguka juu ya jiwe hilo atavunjwa vipandevipande.

Neno "jiwe hili" nijiwe sawa na lile la 21:42. Hii ni sitiari inayomaanisha kuwa Kristo atamharibu mtu yeyote anayempinga. "Jiwe litamvunjavunja yeyote anayeanguka juu yake"

Kwa yeyeote litayemwangukia litamsaga

Hiki ni krai kinachoonesha kuwa Kristo ndiye atakuwa hakimu wa mwisho na atamharibu kila mtu atakayempinga.

Matthew 21:45

Sentensi unganishi

Viongozi wa dini wanamwinukia Yesu juu ya mfano ambao Yesu alifundisha

Mifano yake

Mifano ya Yesu

Matthew 22

Mathayo 22 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Some translations set poetry farther to the right than the rest of the text to show that it is poetry. The ULB does this with the poetry in verse 44, which is from the Old Testament.

Dhana maalum katika sura hii

Wedding Feast

In the parable of the wedding feast (Matthew 22:1-14), Jesus taught that when God offers to save a person, that person needs to accept the offer. Jesus spoke of life with God as a feast that a king prepares for his son, who has just gotten married. In addition, Jesus emphasized that not everyone whom God invites will properly prepare themselves to come to the feast. God will throw these people out from the feast.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Maana iliyodokezwa

Kama waandishi wengine wa Injili, Mathayo anadhani kwamba wasomaji wake wataelewa hali nyingi ambazo anawasilisha, kwa hiyo hatoi maelezo mengi. Anasema, kwa mfano, katika Mathayo 22:15-22, kwamba Wafarisayo walijaribu kumdanganya Yesu ili aseme mambo mabaya, lakini anadhani kwamba wasomaji wataelewa kwa nini swali lao kwa Yesu lilikuwa la hatari kujibu (Mathayo 22:16) ). Walitarajia kwamba Yesu katika jibu lake angewakasirisha Wayahudi au mamlaka ya Kirumi.

Kitendawili

Kitendawili ni taarifa inayoonekana kuwa ya ajabu, ambayo ni kana kwamba inajikana yenyewe, lakini kwa hakika sio ya ajabu. Katika sura hii, Yesu ananukuu Zaburi ambapo Daudi anamwita mwanawe "bwana," yaani, mkuu. Wayahudi daima walitarajia kwamba mababu wangekuwa wakubwa kuliko wazao wao. Katika kifungu hiki, Yesu anajaribu kuwaongoza wasikilizaji hatua kwa hatua kuelewa ukweli kwamba Masihi mwenyewe atakuwa Mungu, na kwamba yeye, Yesu, kwa hakika ndiye Masihi. (Mathayo 22:43-44)

<< | >>

Matthew 22:1

Sentensi unganishi

Kuwakemea viongozi wa dini na kuonesha kutokuamini kwao, Yesuanafundisha mfano wa sherehe ya harusi

nao

"watu"

Ufalme wa mbinguni unafanana na.

Tazama 13:24

Wale wote waliokuwa wamealikwa.

"Watu ambao mfalme alikuwa amewaalika."

Matthew 22:4

Sentensi unganishi

Yesuanaendelea kuelezea mfano

watumishi wengine, akisema waambieni wote walioalikwa

akawaamuru, watumishi wawaambie wale aliowaalika.

Angalieni

"Angalia" au "Sikiliza" au "Kuwa msikivu kwa kile ninachotaka kukuambia."

Fahali na ndama wangu wameuawa

Inamaanisha kuwa wale wanyama wameshapikwa na wako tayari kwa kuliwa. "Watumishi wangu wamechinja na wamewapika mafahali na ndama wangu wanono"

Mafahali na ndama wangu wanono

"Mafahali wangu na ndama wangu walio wazuri kwa kula"

Matthew 22:5

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuelezea mfano

Hawakuzingatia kwa dhati.

"Lakini wale wageni walioalikwa na mfalme walipuuzia"

akawaua wale wauaji

Inamaanisha kuwa, askari wa mafalme waliawaua wale wauaji.

Matthew 22:8

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuelezea mfano

walioalikwa

"Wale ambao nimewaalika"

Makutano ya njia kuu.

"Mahali ambapo barabara hukutana." mfalme anawatuma watumishi kwenye maeneo ambayo wana uhakika mkubwa wa kupata watu.

wema na wabaya

"watu wabaya na watu wema"

Hivyo ukumbi wa harusi ulijaa watu

"kwa hivyo wageni waliujaza ukumbi wa harusi"

ukumbi

chumba kikubwa

Matthew 22:11

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuelezea mfano

ulipataje kufika hapa ndani bila vazi la harusi?

"haujavaa vazi rasmi kwa ajili ya harusi. haupaswi kuwa hapa"

mtu huyo hakujibu kitu chochote

"yule mtu alikuwa kimya"

Matthew 22:13

Sentensi unganishi

Yesu anahitimisha mfano wa harusi

mfungeni mtu huyu mikono na miguu

"mfungeni kiasi kwamba hawezi kusogeza mikono na miguu"

nje katika giza kuu

Tazama 8:11

kilio na kusaga meno

Tazama 8:11

Kwa kuwa watu wengi wanaitwa lakini wateule ni wachahe

"Kwa kuwa Mungu huwakaribisha watu wengi, lakini huchagua wachache"

kwa

Neno hili linamaaisha mpito. Yesu anamaliza mfano na sasa ataeleza maana ya mfano

Matthew 22:15

Sentensi unganishi

Hii inaanzisha habari ya viongozi wa dini wakipanga jinsi ya kumkamata Yesu kwa kutumia maswali mengi magumu. Hapa Mafarisayo wanamuuliza Yesu juu ya kulipa kodi kwa Kaisari.

Jinsi ya kumkamta Yesu katika maneno yake mwenyewe.

"Jinsi ambavyo wangeweza kumsababisha Yesu kukosea katika kauli ili wamkamate"

wanafaunzi wao ... Maherode

Wanafunzi wa Mafarisayo walikubaliana na swala kulipa kodi kwa mamlaka za Kiyahudi. Maherode walikubaliana na swala la kulipa kodi kwa mamlaka za Kirumi. kwa maana hiyo, Mafarisayo waliamini kuwa kwa vyote ambavyo Yesu angejibu; angelikosea moja ya makundi hayo.

Maherode

Hawa walikuwa wafuasi na maofisa wa Herode mfalme wa Wayahudi. Alikuwa rafiki wa mamlaka za Kirumi.

Hauoneshi upendeleo kwa watu.

"Huoneshi heshima ya kipekee kwa baadhi ya watu" au " haujali tu watu maarufu zaidi."

Kulipa kodi kwa kaisari

Watu hawakulipa kodi moja kwa moja kwa Kaisari lakini kwa mmoja wa maofisa wake. "Kulipa kodi ambayo Kaisari alilitaka"

Matthew 22:18

Kwa nini mnanijaribu, enyi wanafiki?

"msinijaribu mimi enyi wanafiki" au "Najua kuwa ninyi wanafiki mnajaribu kunijaribu!"

Dinari.

Sarafu ya kirumi yenye thamani ya ujira wa siku.

Matthew 22:20

wa

kiwakilishi "wa" kinamaanisha Maherode na wanafunzi wa Mafarisayo.

Sura na jina hili ni vya nani

Niambieni sura na jina mnavyoviona kwenye hii sarafu ni vya nani?

vya Kaisari.

"Sarafu hii ina sura na jina la Kaisari"

vitu ambavyo ni vya Kaisari

"Vitu ambavyo ni mali ya Kaisari"

Vitu ambavyo ni vya Mungu.

"Vitu ambavyo ni mali ya Mungu."

Matthew 22:23

Sentensi unganishi

Masadukayo wanajaribu kumkamata Yesu kwa kumtega kwa swali gumu kuhusu ndoa na ufufuo wa wafu.

Mwalimu, Musa alisema, 'ikiwa mtu amekufa.

Walikuwa wakimuuliza kuhusu alichoandika Musa katika Maandiko. "Musa alisema kwamba ikiwa mtu amekufa."

Ndugu yake...mke wake...ndugu yake.

Kimilikishi "yake" inamaanisha yule mfu

Matthew 22:25

Sentensi unganishi

Mafarisayo wanaendelea kumwuliza Yesu swali

wa kwanza ... wa pili ... wa saba

namba za mpangiliio

Baada ya wote.

"Baada ya kila ndugu kuwa amemuoa" au " Baada ya kila ndugu kuwa amefariki."

baada ya kufanya hivyo wote

"baada ya kila ndugu kufa"

sasa

Hapa Masadukayo wanabadilisha habari ya ndugu yule wa saba na kuuliza swali halisi

Matthew 22:29

Mnakosea

"Mnakosea juu ya ufufuo"

Nguvu za Mungu.

"Kile ambacho Mungu anaweza kufanya."

katika ufufuo

"wakati wafu watapofufuka"

hawaoi

"watu hawataoa"

wala kuolewa

"wala watu hawataruhusu watoto wao kuolewa"

Matthew 22:31

Sentensi unganishi

Katika 22:32, Yesu ananukuu kutoka kitabu cha Kutoka ili kuhakikisha kuwa watu wataishi tena baada ya kifo

Hamjasoma kile ambacho ...Yakobo?'

"Najua mmekwisha soma, Lakini inaonekana hamkuelewa ambacho...Yakobo.'

Kile kilichosemwa kwenu na.

"Kile alichowaambia Mungu"

Mungu, anasema, Mimi ni...Yakobo?'

"Mungu alimwambia Musa kwamba Yeye, Mungu, ni Mungu wa Abramu,Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo."

"Si Mungu wa wafu balini Mungu wawalio hai

wa wafu, bali ni Mungu wa walio hai"

Matthew 22:34

Sentensi unganishi

Farisayo mwanasheria alimtega Yesu kwa swali kwa kumwuliza swali gumu juu ya amri kuu

Mwanasheria.

Farisayo ambaye alikuwa na ujuzi maalum katika kuelewa sheria ya Musa.

Matthew 22:37

Maelezo kwa ujumla

Yesu ananukuu ile amri kuu kutoka Kumbukumbu la torati

kwa moyo wako wote, na kwa akili zako zote. na kwa roho yako yote.

Virai vyote vitatu vinamaanisha kitu kilekile. Vinamaanisha kuwa mtu lazima ampende Mungu kwa pendo la ndani na kwa kujito kwa ukweli.

.kuu na ya kwanza

Neno "kuu" na ya "kwanza" yanamaanisha kitu kilekile. vinasisitiza kuwa hii ni amri ya muhimu

Matthew 22:39

Maelezo kwa ujumla

Yesu ananukuu mstari toka Walawi kama amri kuu ya pili

Na ya pili inafana na hiyo

Yaweza kumaanisha 1) "kuna amri ya pili ambayo inafuatia kwa umuhimu" au 2) "kuna amri ya pili ambayo nayo ni ya muhimu." Kwa namna yeyote ile, Yesu anamaanisha kuwa amri hizi zote ni za muhimu kuliko amri zingine zote.

Na amri ya pili

Ya pili ni katika kupangilia

inafanana

Tazama 2:37

jiraniyako

Neno "jirani" inamaana zaidi ya mtu aliye karibu na wewe. inamaanisha kuwa mtu lazima awapende watu wote

Sheria zote na Manabii hutegemea hutegemea amri hizi mbili

Neno "sheria zote na manabii" limzznisha maandiko yote. "Kila kitu ambacho Musa na Manabii waliandika katika maandiko zinategemea amri hizi zote mbili"

Matthew 22:41

Sentensi unganishi

Yesu anawauliza Mafarisayo swali gumu ili kuzuia mpango wao wa kumkamata.

Sasa

Neno hili limetumika ili kuonesha mwanzo wa habari mpya. Mathayo anaanza kueleza sehemu mpya ya simulizi wakati Yesu alipowauliza viongozi wa dini swali.

Mwana ... mwana wa Daudi

vyote hivi "mwana" vinamaanisha "kizazi"

Matthew 22:43

Maelezo kwa ujumla

Yesu ananukuu toka Zaburi kuonesha kuwa Kristo ni zaidi ya "mwana wa Daudi"

Ni kwa namna gani Daudi katika Roho anamwita Bwana

"Yesu anatumia swali kuwafanya viongozi wa dini kufikiri kwa undani zaidi juu ya Zaburi anyotaka kuinukuu "Niambieni kwa nini Daudi katika Roho anamwita Bwana"

Daudi katika Roho

"Daudi ambaye anavuviwa na Roho. "Hii inamaanisha kuwa Roho Mtakatifu anamwezesha Daudi kusema.

anamwita

Hapa "mwi" inasimama badala ya Kristo, ambaye pia ni kizazi cha Daudi.

Bwana alimwambia

Neno "Bwana" inamaanisha Mungu Baba

Katika mkono wangu wa kuume,

Kiwakilishi "wangu" kinamaanisha Mungu Baba. "Mkono wa kuume" huwa inatumika kuonesha sehemu ya heshima

Hadi nitakapowaweka maadui zako wawekwe chini ya miguu yako

Hii ni nahau. "hadi nitakapowashinda adui zako" au hadi nitakapowafanya maadui zako kukuinamia"

Matthew 22:45

Sentewnsi unganishi

Huu nu mwisho wa jitihada za viongozi wa dini kutaka kumkamata Yesu kwa maswali mengi

Maelezo kwa ujumla

Huu ni mwisho wa sehemu ya habari hii inayoanzia 19:1, ambayo inaelezea habari za Yesu akihudumia Yuda

Kama Daudi anamwita Kristo "Bwana," kwa namna gani awe mtoto wa Daudi?

"Daudi anamwita Yeye Bwana, kwa hiyo Kristo lazima awe zaidi kuliko mzao wa Daudi."

Kama Daudi tena anamwita Kristo.

Daudi amemrejea Yesu kama "Bwana" kwa sababu Yesu hakuwa tu mzao wa Daudi, lakini pia alikuwa bora kuliko Daudi.

kumjibu neno

"Neno" inamaanisha kile amabacho watu husema. "kumjibu yeye chochote" au " kumjibu"

maswali zaidi

Inamaanisha kuwa hakuna aliyemuuliza maswali ya jinsi hiyo ambayo yalikusudiwa kuwaYesu angeyajibu kimakosa ili viongozi wa dini wamkamate

Matthew 23

Mathayo 23 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Wanafiki

Unafiki wa Wafarisayo ni neno kuu katika sura hii. Yesu anazungumzia kwa kina kuhusu unafiki huu. Wafarisayo waliunda sheria ambayo hakuna mtu angeweza kutii, na kisha wakawashawishi watu kwamba walikuwa na hatia kwa sababu ya kutotii sheria. Pia, sheria za Wafarisayo ziliwapa sababu za kutotii amri za asili za Mungu za Sheria ya Musa.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Kutusi

Katika tamaduni nyingi, ni makosa kuwaalumu watu. Maneno mengi katika sura hii yaliyowalenga Wafarisayo yanaweza kuchukuliwa kama matusi. Wanaitwa "wanafiki," "viongozi vipofu," "wajinga," na "nyoka." Yesu anatumia maneno haya kuelezea na kuhukumu tabia zao.

Kitendawili

Kitendawili ni taarifa inayoonekana kuwa ya ajabu, ambayo ni kana kwamba inajikana yenyewe, lakini kwa hakika sio ya ajabu. Kwa mfano, "aliye mkuu kati yenu atakuwa mtumishi wenu" (Mathayo 23:11-12).

<< | >>

Matthew 23:1

Maelezo kwa ujumla

Huu ni mwamnzowa habari mpya inyoenedelea hadi 25:44, amabpo Yesu anafundisha juu ya wokovu na hukumu ya mwisho. Anaanza kuwaonya watu juu ya Mafarisayo na waandishi

Wanakalia kiti cha Musa.

Kiti kinamaanisha mamlaka ya kutawala na kuhukumu. "Wanayo mamlaka kama aliyokuwanayo Musa." au "wanayo mamlaka ya kusema maana ya sheria Musa."

Chochote.

"Yoyote" au "kila kitu."

Matthew 23:4

Wanafunga mizigo mizito ambayo ni migumu kubeba, na kisha kuwabebesha watumabegani

"Wanawawekea ninyi kanuni nyingi ambazo ni ngumu kufuata."

Wao wenyewe hawasogezi hata kidole kuibeba

"Wao hawatatoa msaada hata msasada kidogo"

Matendo yao yote huyafanya ili watazamwe na watu

wanafanya mataendo yao kwa kusuadi la kutazamwa na watu

Kwa sababu wao hupanua masanduku yao, na huongeza ukubwa wa mapindo wa mavazi yao

Hivi vyote ni vitu ambavyo Mafarisayo huvifanya ili waonekane kuwa wanamtii Mungu kuliko watu wengine

Masanduku

Haya ni makasha madogo ya ngozi yenye karatasi za maandiko

hongeza ukubwa wa mapindo ya mavazi yao

Mafarisayo huweka mapindo marefu chini ya kanzu zao kuonesha uchaji wao kwa Mungu.

Matthew 23:6

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuongea na makutano kuhusu Mafarisayo

maeaneo ya kifahari ... viti vya heshima

Maeneo yaote haya na yale amabayo watu muhimu hukaa

maeneo ya sokoni

Maeneo makubwa ya wazi amabyo watu huuza na kununua bidhaa

na kuitwa 'Rabi' na watu

"ili watu wawaite rabi"

Matthew 23:8

Lakini ninyi hampaswi kuitwa

"Msimruhusu mtu yeyote awaite"

ninyi

viwakilishi vyote vya "ninyi" viko katka wingi na vinamaanisha wafauasi wote wa Yesu

wote ni ndugu

Neno "ndugu" linamaanisha "waumini wenzenu"

msimwite mtu yeyeote hapa duniani kuwa baba

"msiseme kwamba mtu yeyote hapa duniani ni baba yenu"

kwa kuwa mnaye baba mmoja tu

"baba" ni cheo muhimu cha Mungu

walla msije mkaitwa

"pia msimruhusu mtu kuwaita"

Kwa kuwa mnaye mwalimu mmoja tu, yaani Kristo

Wakati Yesu aliposema "Kristo" alikuwa anasema juu yake mwenyewe katika nafsi ya tatu. AT: "Mimi, Kristo ndiye mwalimu wenu pekee."

Matthew 23:11

Bali aliye mkubwa miongoni mwenu

"mtu maarufu miongono mwenu"

miongoni mwenu

kiwakilishi "mwenu" ni cha wingi na kinamaanisha wafuasi wa Yesu

Yeyote ajiinuaye

"ajifanyaye mwenyewe kuwa maarufu."

atashushwa

"Mungu atamshusha

atainuliwa

Mungu atamuheshimu

Matthew 23:13

Sentensi unganishi

Yesu anaanza kuwakemea viongozi wa dini kwa sababu ya unafiki wao

Lakini ole wenu

tazama 11:20

Mnawaffungia watuufalme wa mbinguni

"Mnawazuia watu kumpokea Mungu wetu wa mbinguni kuwa mfalme wao"

Hamwezi kuingia

"Hamumruhusu Mungu kuwa mfalme wenu"

na hamuwaruhusu wanaoingiakufanya hivyo

"wala hamuwarusu wale wanaotaka kumpokea Mungu kuwa mfalme wao kufanya hivyo"

"mnasafiri umbali mrefu"

kumfanya mtu mmoja aamini

"kumfanya mtu mmoja aamini dini yenu"

mwana wa jehanamu

"Mtu ambaye mahali pake ni kuzimu." au mtu ambaye hanabudi kwenda kuzimu."

mnawameza wajane wajane.

"Kuiba kila kitu kutoka kwa wanawake wasio na wanaume wa kuwalinda."

Matthew 23:16

Viongozi vipofu...wapumbavu.

Tazama 15:12

kwa hekalu, si kitu

"kwa hekalu hawezi kulinda kiapo chake

Amefungwa na kiapo chake.

"Lazima atende kile alichoahidi kufanya."

Kipi ni kikubwa kuliko kingine, dhabu, au hekalu ambalo limeweka wakfu dhahabu ya Mungu?

Hekalu amablo limetumika kuweka wakfu dhahabu kwa Mungu ni la muhimu kuliko dhahabu ile"

Hekalu amabalo limeweka wakfu dhahabu

"Hekalu ambalo hutengeneza dhahabu ni mali ya Mungu pekee"

Matthew 23:18

Na

"na ninyi pia husema"

si kitu

"hakuna haja ya kulinda kiapo chake"

sadaka

ni mnyama au nafaka ambayo mtu anaweza kuileta kwa Bwana na kuiweka madhabahuni

amefungwa na kiapo chake

"lazima afanye kile alichoahidi kufanya"

Watu vipofu.

Viongozi wa Kiyahudi walikuwa vipofu kiroho. Ingawa walijidhania kuwa walimu, hawakuwaeza kuuelewa ukweli wa Mungu

Kipi ni kikubwa kuliko kingine, sadaka, au madhabahu ambayo huweka wakfu sadaka zinazotolewa kwa Mungu?

"Madhabahu ambayo huzifanya sadaka kuwa takatifu ni kuu kuliko sadaka

"madhabahu ambayo huweka wakfu sadaka"

madhabahu ambayo huziweka sadaka kuwa rasmi kwa Mungu"

Matthew 23:20

na kwa vitu vyote vilivyo juu yake

"kwa vitu vyote ambvyo sadaka zote huwekwa juu yake"

na kwa yeye akaaye ndani yake ... na kwa yeye aketiye juu yake

virai vyote hivi vinamaanisha Mungu Baba.

Matthew 23:23

Ole wenu.

Tazama 11:20.

Bizali, Mnanaa, na Mchicha.

Majani na mbegu zinazotumika kuungia chakula.

kuacha mengine bila kutekeleza

"hamkutii

mambo mazito

"mambo y a muhimu zaidi"

lakini haya mnapaswa kuwa mmeyafanya

"mnapaswa kuwa mmeziheshimu hizi sheria za muhimu"

na siyo kuyaacha mengine bila kuyatekeleza

"wakati pia mnatii zile sheria ndogondogo"

Ninyi viongozi vipofu.

Tazama 15:12

Ninyi ambao mnachuja mdudu mdogo lakini mnameza ngamia.

Kuwa mwaangalifu kufuatilia sheria zenye uzito kidogo na kupuuzia sheria zenye uzito mkubwa, hiyo ni upumbavu sawa na kuwa mwangalifu kwa kutokumeza mnyama mdogo aliye najisi, bali unakula nyama ya mnyama mkubwa sana aliye najisi pengine kwa makusudi au kwa kutokujuwa. AT: "Wewe ni mpumbavu kama mtu ambaye anachuja mdudu aliyeangukia ndani ya kinywaji chake lakini akimeza ngamia."

Kuchuja mdudu.

Kujucha kwa kutumia ktambaa ili kuondoa mdudu katika kinywaji

Mdudu.

Mdudu mdogo arukae.

Matthew 23:25

Ole wenu.

Tazama 11:20

Kwa kuwa mnasafisha nje ya kikombe a nje ya sahani... kutokuwa na kiasi

"Waandishi" na "Mafarisayo" kwa wengine wanaonekana "safi kwa nje, lakini ndani ni wachafu

Kwa ndani wamejaa dhuluma and kutokuwa na kiasi.

"Wanachukua vitu vya watu kwa ubinafsi

Ewe Mfarisayo kipofu.

Mafarisayo walikuwa vipofu kiroho. Ingawa wao wenyewe walijidhania kuwa walimu. hawakuwa na uwezo wa kuelewa ukweli wa Mungu

Safisheni kwanza ndani ya kikombe na ndani ya sahani, ili nje pia pawe safi.

Hii ni sitiari inayomaanisha kuwa kama wangekuwa safi mioyoni mwao, basi matokeo yake wangekuwa safi kwa nje pia

Matthew 23:27

kwa kuwa mnafanana na makaburi yaliyopakwa chokaa... kichafu

hii ni kejeli inayoonesha kuwa Mafarisayo na waandishi wanaonekana kuwa safi nje, lakini ndani ni wachafu

makaburi yaliyopakwaa chokaa

"makaburi ambayo mtu ameyapaka chokaa" Wayahudi walipakaa makaburi kwa chokaa ili kuepusha kuyagusa. Kugusa kaburi ilihesabiwa kuwa ni unajisi.

Matthew 23:29

ya wenye haki

"ya watu wenye haki"

siku za baba zetu

"wakati wa mababu zetu"

tusingekuwa tumeshiriki pamoja nao

"tusingekuwa tumeshirikiana nao"

kumwaga damu

Damu inamaanisha uhai. kumwaga damu inamaanisha kuua. "kuua" au "mauaji"

watoto wa hao

"watoto inamaanisha uzao"

Matthew 23:32

Pia ninyi mnakamilisha kujaza sehemu inayostahili dhambi ya baba zenu.

"Ninyi mna kamilisha dhambi ambazo babu zenu walizianzisha,"

Enyi nyoka, enyi wana wa vipiribao.

"Ninyi ni waovu na hatari kama nyoka wenye sumu."

wana wa vipiribao

tazama 3:7

Jinsi gani mtaepuka hukumu ya jehanamu?

"Hakuna njia mnayoweza kutumia kuepuka hukumu ya jehanamu!"

Matthew 23:34

nawatuma

"nitawatuma." Hapa "ni" inamaanisha Yesu.

juu yenu patatokea damu zote za wenye haki zilizomwagwa duniani

"Mungu atawahukumu kwa mauaji ya watu wenye haki"

kuanzia damu ... kwa damu

"kutoka mauji hadi ... mauaji"

Kutoka...Abeli...to...Zekaria.

Abeli alikuwa mhanga wa kwanza katika mauaji, na Zakaria huenda akafikiriwa kuwa wa mwisho kuuwawa na Wayahudi hekaluni.Watu hawawaili wanawakilisha mauaji ya watu wote wenye haki

Zakaria.

Siyo baba yake na Yohana Mbatizaji.

mliyemuua

Yesu hamaanisha watu wale aliokuwa akisema nao kuwa ndio waliomua Zekaria. Anamaanisha kuwa mababu zao ndio waliomuua.

Kweli nawaambieni

"Nawaambia ukweli." Hii inaongeza msisitizo wa kile Yesu atakachosema baadye.

Matthew 23:37

Sentensi unganishi

Yesu anaomboleza juuya watu wa Yerusalemu kwa sababu wanamkataa kila aliyetumwa na Mungu kwao

Yerusalemu, Yerusalemu.

Yesu anazungumza na watu wa Yerusalemu kana kwamba wao wenyewe ndio walikuwa mji.

ambao wanatumwa kwako

wale ambao Mungu huwatuma kwako

Watoto wenu.

"watu wako" au 'kizazi chako"

kama vile kuku awakusanyavyo vifaranga wake chini ya mabawa yake

Huu ni usemi unaosisitiza upendowa Yesu kwa watu n a jinsi alivyotaka kuwajali.

Nyumba yako imeachwa ukiwa.

"Mungu ataiacha nyumba yako, na itabaki tupu."

Nyumba yako.

Maana yake ni : (1). Mji wa Yerusalemu au (2). Hekalu.

Nami nakuambia

Huu ni msisitizo wa kile Yesualichosema baadaye

Amebarikiwa yeye ajaye kwa jina la Bwana

Tazama 21:9

Matthew 24

Mathayo 24 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Katika sura hii, Yesu anaanza kutabiri kuhusu wakati ujao kutoka wakati huo hadi atakaporudi kama mfalme wa ulimwengu. (Angalia: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#prophet)

Dhana maalum katika sura hii

"Mwisho wa ulimwengu"

Katika sura hii, Yesu anatoa jibu kwa wanafunzi wake wakati wanauliza jinsi watakavyojua wakati atakapokuja tena. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#writing-apocalypticwriting)

Mfano wa Nuhu

Katika wakati wa Nuhu, Mungu alituma gharika kuu kuwaadhibu watu kwa dhambi zao. Aliwaonya mara nyingi kuhusu kuja kwa mafuriko hayo, lakini kwa hakika yalianza ghafla. Katika sura hii, Yesu analinganisha mafuriko hayo na siku za mwisho. (Angalia: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Ruhusu"

ULB hutumia neno hili kuanzisha amri kadhaa za Yesu, kama "wacha wale walio Yudea wakimbilie milimani" (24:16), "yule aliye juu ya nyumba asije akashuka kuchukua chochote kutoka kwa nyumba yake "(24:17), na" aliye mashambani asirudi kuchukua nguo yake "(24:18). Kuna njia nyingi za kuunda amri. Watafsiri wanapaswa kuchagua njia za asili zaidi katika lugha zao wenyewe.

<< | >>

Matthew 24:1

Sentensi unganishi

Yesu anaanza kueleza matukio amabayo yatakuja tokea kabla hajarudi mara ya pili

alitoka hekaluni

Inaonesha kuwa Yesu hakuwa ndani ya hekalu. alikuwa kwenye korido la hekalu.

Je, hamyaoni mambo haya yote?

"Ngoja niwaambie kitu fulani kuhusu majengo haya yote."

kweli nawambia

"Nawaambia ukweli." huu ni msisitizo wa kile alichosema Yesu badaye

Hakuna jiwe litakalobaki juu ya jiwe lingine ambalo halitabomolewa

"wakati maaskari walio adui watakapokuja, watabomoa kila jiwe juu ya majengo haya"

Matthew 24:3

kitu gani kitakuwa dalili ya kuja kwako na mwisho wa ulimwengu

Neno "kuja kwako" linamaanisha wakati Yesu atakapokuja katika nguvu, kuanzisha utawala wa Mungu duniani na kukifikisha kizazi hiki mwisho wake.

Mwe waangalifu asije mtu akawapotosha.

"Mwe waangalifu kwamba msiamini yeyote ambaye atawaongopea kuhusu mambo haya."

wengi watakuja kwa jina langu

Neno "jina" linamaanisha "katika mamlaka" au " kama mwakilishi" wa mwingine. "Wengi watadai kuwa wamekuja kama wawakilishi wangu" au "wengi watasema kuwa wanaongea kwa niaba yangu"

Matthew 24:6

Angalieni msiwe na wasiwasi.

"Msije mkaruhusu mambo haya kuwapa wasiwasi."

kwa kuwa taifa litainuka juu ya taifa jingine, na ufalme dhidi ya ufalme

Hii inamaanisha kitu kilekile. na msisitizo wake ni kwamba kutakuwa na mapigano kila mahali

ni mwanzo tu wa uchungu

Hii inamaanisha maumivu mwanamke huyapata wakati anapotaka kujifungua mtoto. Sitiari hii inamaanisha kuwa haya matetemeko, njaa na vita ni mwanzo tu wa matukio yatakayotuongoza kuelekea mwisho wa dunia

Matthew 24:9

Watawatoa kwa ajili ya mataeso na kuwaua

"watuwatawatoa kwa mamlaka amaboa watawatesa na kisha kuwaua"

mtatchukiwa na mataifa yote

"watu kutoka kilataifa watawachukia"

kwa sababu ya ina langu

"kwa sababu mnaniamini "

watatokea

"watakuja"

Matthew 24:12

uovu utaongezeka

"watu watafanya dhambi zaidi na zaidi"

Upendo wa wengi utapoa.

Maana ya karibu: 1."watu wengi hawatawapenda wenzao." au 2."watu wengi hawatampenda Mungu."

atakayevumilia

"yeyote atayebaki na uvumilivu"

mpaka mwisho

haieleweki kama "mwisho" inamaanisha mtu anapokufa, au wakati dhiki itakapokoma, au mwisho wa nyakati wakati Mungu atakapojionesha kuwa mfalme. jambo l a kuzingatia hapa ni uvumilivu usiokoma

ataokolewa

"Mungu atamwokoa mtu huyo"

Hii injili ya ufalme itahubiriwa

"Watu watahubiri ujumbe juu ya utawala wa Mungu"

Mataifa yote.

"Watu wote katika sehemu zote."

na ndipo ule mwisho

"mwisho wa ulimwengu" aua "mwisho wa nyakati"

Matthew 24:15

chukizo la uharibifu

"mtu wa aibu atakayevinajisi vitu vya Mungu"

Lililosemwa na nabii Danieli.

"Kuhusu ambacho nabii Danieli aliandika."

asomaye na afahamu

Haya maneno hayakusemwa na Yesu. Matahayo aliongezea haya ili kupata usikivu

Na yule aliyeko juu ya paa

mapaa wakati wa Yesu yalikuwa tambarare, kiasi kwamba watu wangeweza kusimama

Matthew 24:19

Wao ambao wana mtoto.

"wanawake wenye mimba"

katika siku hizo

"wakati huo"

kukimbia kwenu kusiwe

"kwamba msikimbie"

Wakati wa baridi.

"Majira ya baridi."

kama siku hizo zisingefupishwa, hakuna ambaye angeokoka

"kama Mungu hatazifupisha siku zadhiki watu wote wangekufa"

Wenye mwili

Watu.

siku hizo zitafupishwa

"Mungu atazifupisha siku za dhiki"

Matthew 24:23

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwaambia wanafunzi wake

Msiamini maneno hayo

"Msiamini mambo ya uongo wanayowaambia."

kwa kusudi la kuwapotosha

"ili kuwafanya watu wasitii"

kupotosha, kama ingeliwezekana hata na wateule

"kupotosha, kama ingeliwezekana, watawafanya hata na wateule kutotii"

Matthew 24:26

ikiwa watawambia, 'Kristo yuko jangwani,' msiende huko jangwani. Au 'Tazameni, 'yuko ndani ya nyumba,'

"au, kama mtu atawambia kuwa Kristo yumo ndani ya nyumba"

ndani ya nyumba

"ndani ya chumba cha siri"

kama vile radi inavyomulika ... ndivyo itavyokuwa kuja

Hiiinamaanisha mwana wa mtu atakuja kwa kasi sana na itakuwa rahisi kumwona

Kama vile radi inavyomulika...ndivyo itakavyokuwa kuja.

Atakuja kwa kasi na itakuwa rahisi kuonekana.

mwana wa Adamu

Yesu anaongea juu yake katika nafsi ya tatu

Popote ulipo mzoga, huko ndiko tai wakusanyikapo.

Maana ya karibu ni: (1). Mwana wa Adamu atakapokuja, kila mtu atamuona na kujua kwamba amekuja; (2). Popote walipo watu aliokufa kiroho, manabii wa uongo watakuwepo huko kuwaambia uongo.

tai

Ndege ambao wanakula mizoga au wanyama wanaokaribia kukata roho.

Matthew 24:29

Lakini mara

"wakati huo"

dhiki y a siku hizo

"wakati huo wa dhiki"

Jua litatiwa giza.

"Mungu atalifanya jua liwe giza."

Nguvu za mbinguni zitatikisika.

" Mungu atatikisa vitu katika mbingu na juu ya anga."

Matthew 24:30

Mwana wa Adamu ... mwo ... wake

Yesu anaongea juu yake katika nafsi ya tatu.

makabila yote

watu wa makabila yote

atawatuma malaika wake kwa sauti kuu ya tarumbeta

"wakati tarumbeta itakapolia atawatuma malaika wake"

Watakusanya.

"Malaika wake watakusanya."

Wateule wake.

Watu ambao Mwana wa Adamu amewachagua.

kutoka pande nne za dunia, kutoka mwisho wa mmoja wa mbingu hadi mwingine

kutoka kila upande

Matthew 24:32

amekaribia

"wakati wangu wa kuja umekaribia"

Karibu na malango.

karibu na malango

Matthew 24:34

kweli nawaambia

"Nawaambia ukweli" huu ni msisitizo wa kile kinachosemwa baadaye

Kizazi hiki hakitapita.

"Watu wanaoishi kipindi hiki hawatafariki wote."

Hadi mambo yote haya yatakuwa yametokea.

"Mpaka Mungu asababishe mambo haya yote yatimie."

Mbingu na nchi zitapita.

"Mbingu na nchi hazitaendelea kuwapo."

maneno yangu hayatapita kamwe

"kile ninachosema daima kitabaki kuwa ukweli"

Matthew 24:36

siku ile na saa

hapa "siku" na "saa" vinamaanisha muda halisi ambao mwana wa Adamu atarudi

Wala Mwana.

"Hakuna hata mwana"

mwana

Hiki ni cheo muhimu cha Yesu, Mwana wa Mungu

Baba

Hiki ni cheo muhimu cha Mungu

Matthew 24:37

Kama ilivyokuwa katika siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa kuja kwa Mwana wa Adamu.

"Siku ambayo Mwana wa Adamu atakuja tena itakuwa kama ilivyokuwa siku za Nuhu,"

Mwana wa Adamu

Yesu anaongea juu yake akaitumia nafsi ya tatu

katika safina na hawakujua kitu

"katika safina. Na watu hawakuju kuwa kuna kitu kilikuwa kinaenda kutokea"

ndivyo itakavyokuwa kuja kwa Mwana wa Adamu

"Hivyo ndivyo itakavyokuwa wakati wa kuja kwa Mwana wa Adamu"

Matthew 24:40

Sentensi unganishi

Yesu anaanza kuwaambia wanfunzi wake kuwa tayari kwa ajili ya kurudi kwake

Ndipo.

Wakati Mwana wa Adamu ajapo.

Mmoja atachukulia, na mmoja ataachwa nyuma.

Maana za karibu: 1. Mungu atamchukuwa mmoja kwenda mbinguni na ataacha mmoja duniani kwa ajili ya adhabu, au 2. Malaika watamchukua mmoja kwa ajili ya adhabu na kumuacha mwingine kwa ajili ya baraka.

Kinu.

Chombo cha kusagia.

Kwa hiyo.

"Kwa sababu ya kile nilicho waambia."

Kuweni macho.

Kaa tayari.

Matthew 24:43

ikiwa bwana mwenye nyumba ... nyumba yake kuvamiwa

Yesu anaatumia mfano wa bwana na mtumwa kufafanua kuwa wansfunzi wake wanatakiwa kujiandaa kwa ajili ya kurudi kwa Yesu

Mwizi.

Yesu anasema atakuja wakati ambao watu hawamtarajii, siyo kwamba atakuja kuiba.

Angekuwa amelinda.

"Angelinda nyumba yake" kuisalimisha.

Na asingeruhusu nyumba yake ivamiwe.

"Asingeruhusu mtu yeyote kuingia ndani ya nyumba yake aibe vitu."

Mwana wa Adamu

Yesu anatumia nafasi ya tatu kujisemea yeye

Matthew 24:45

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea na mithali yake ya bwana na mtumwa kufafanua kuwa wanafunzi wake wanapaswa kujiandaa kwa ajili y a kurudi kwa Yesu.

Hivyo ni nani mwaminifu, mtumwa mwenye akili, ambaye bwana wake...wakati?

"Hivyo ni nani mwaminifu, mtumwa mwenye akili? Ndiye yule ambaye bwana wake...wakati."

Awape chakula chao

"Awape watu chakula chao katika mji wa bwana wake"

Kweli nawambia

"Nawaambieni ukweli" Hii inaongeza msisitizo wa kile ambacho Yesu atakuja kusema baadaye.

Matthew 24:48

Sentensi unganishi

Yesu anahitimisha mithali yake ya bwana na mtumwa ...

Anasema moyoni mwake.

"Anafikiri akilini mwake."

Bwana wangu amekawia

Bwana wangu hafanyi haraka kuja

katika siku ambayo hatarjii, na katika saa ambayo haijui

Virai hivi vyote vinamaanisha kitu kilekile. vinasisitiza kuwa bwana atakuja wakati ambao mtumwa wake hamtarajii kuja.

Kumweka katika nafasi au kumhesabu kama.

"Kumtendea"

kumweka katika nafasi

"kumtendea"

atamkata vipande

kumfanya mtu aumie sana

kilio na kusaga meno

Tazama 8:11

Matthew 25

Mathayo 25 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Sura hii inaendeleza mafundisho ya sura ya awali.

Dhana maalum katika sura hii

Mfano wa bikira kumi

Miongoni mwa Wayahudi, wakati ndoa ilipangwa, kulikuwa na muda kabla ya harusi. Mwisho wa muda huo, kijana huyo angeenda nyumbani kwa bibi arusi, ambako alikuwa anamngojea. Sherehe ya harusi basi ingefanyika. Kwa furaha kubwa wangeweza kusafiri hadi nyumba ya bwana harusi, ambako kungekuwa na sikukuu. (Angalia: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#writing-apocalypticwriting)

Yesu anatumia desturi hii kwa kuwaambia mfano wa bikira kumi (Mathayo 25:1-13).

<< | >>

Matthew 25:1

Sentensi unganishi

Yesu anaongea mfano wa wanawali wenyebusara na wale wanawali wajinga kufundisha kuwa wanafunzi wake wanapaswa kujiandaa kwa ajili y a kurudi kwa Yesu

ufslme wa mbinguni utafananishwa na

Tazama 13:24

Lamps.

Hizi ziliweza kuwa, 1.taa zenyewe au mienge iliyotengenezwa kwa kuwekewa kitambaa kuzunguka mwisho wa mti na hulowanishwa na mafuta.

Watano kati yao.

Watano kati ya wanawali.

Hawakuchukua mafuta yoyote.

"Waliyokuwa nayo ni yale tu yaliyokuwa katika taa zao."

Matthew 25:5

Sasa

Neno linaloonesha kuanzisha habari mpya. Yesu anaanza kueleza sehemu ya habari hii.

bwana harusi amechelewa

"wakati bwana harusi alipochukua muda mrefu kuwasili"

Wote walianza kusinzia.

Wanawali wote kumi walianza kusinzia.

kulikuwa na yowe

"mtu mmoja alianza kupiga kelele"

Matthew 25:7

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kueleza mfano

Kutayarisha taa zao.

"Wakarekebisha taa zao ili ziwake kwa mng'ao."

Wapumbavu walisema na welevu.

"Wanawali wapumbavu walisema na wanawali welevu."

Taa zetu zinazimika

"Moto katika taa zetu unaelekea kuzima."

Matthew 25:10

Sentensi ungsnishi

Yesu anahitimisha mfano wa wanawali kumi

wakati wameenda huko

"Wanawali wapumbavu waliondoka."

kununua

"kununua mafuta zaidi"

Wale ambao walikuwa tayari.

Wanawali waliokuwa na mafuta ya ziada.

Mlango ulifungwa.

"watumishi walifunga mlango."

Tufungulie.

"Fungua mlango kwa ajili yetu ili tuingie ndani"

kweli nawaambia

"Nawaambia ukweli" Hiiinatia msisitizo wa kile Yesu alichosema baadaye

"Siwatambui ninyi."

"Si watambui ninyi ni akina nani" au 'si wajui ninyi ni akina nani."

kwa kuwa hamjui siku wala saa

"Hamjui muda halisi ambao Mwana wa Adamu atakuja"

Matthew 25:14

Sentensi unganishi

Yesu anaeleza mfano wa mtumishi mwaminifu na asiye mwaminifu ili kuwafundisha wanafunzi wake kubaki waaminifu wakati yeye hatakuwepo na wawe tayari kwa ajili ya kurudi kwa Yesu.

Ni sawa na.

"Ufalme wa mbinguni ni unafanana na."

Alipotaka kuondoka

"Alipokuwa tayari kuondoka" au mara alipotaka kuondoka."

Aliwakabidhi utajiri wake.

"Akawapa usimamizi wa mali yake." au "akawapa usimamizi wa utajiri wake."

Utajiri wake.

"Mali yake."

Talanta tano.

"Talanta moja" ilikuwa na thamani ya mishahara wa miaka ishirini. Epuka kutafsiri jambo hili katika pesa za siku hizi. Mfano huo unalinganisha uwiano wa kiasi cha tano, cha mbili na kiasi cha moja sawia na kiasi kikubwa cha utajiri uliotumika. "mifuko mitano ya dhahabu."

kulingana nauwezo wake

"kulingana na uwezo wa kila mtumishi wa kusimsmia mali"

Na kuzalisha talanta zingine tano.

"Kutokana na uwekezaji wake, alipata faida ya talanta zingine tano."

na kuzalisha talanta zingine tano

"kutokana na uwekezaji wake, akazalisha talanta zingine tano"

Matthew 25:17

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea mafano wa watumishi na talanta

Alizalisha zingine mbili.

"Alipata faida ya talanta zingine mbili.'

Matthew 25:19

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kueleza mfano wa watumishi na talanta

na baada ya muda

Kirai hiki kimetumika kuonesha mwanzo wa habari mpya. Yesu anaanza kueleza sehemu mpya ya simulizi.

Nimepata talanta tano zaidi

"Nimepata faida ya talanta tano zaidi."

Talanta

Mali yenye thamani kubwa. talanta moja ilikuwa sawa na mishahara ya miaka ishirini.Tazama tafsiri katika. 25:14--15.

Hongera.

"Umefanya kazi vizuri." au "Umefanya vema." Katika utamaduni wako pengine mnao usemi ambao mkuu (mtu mwenye mamlaka) angetumia kuthibitisha kile ambacho mtumishi wake (au yeyote chini yake) amekitekeleza.

Ingia katika furaha ya Bwana wako

"Njoo ufurahie na mimi"

Matthew 25:22

Sentensi unganishi

Yesu anaendelelea kueleza mfano wa watumishi na talanta

Nimepata faida ya talanta zingine mbili

"Nimepata fada ya talanta mbili zaidi"

Umefanya vema

umefanya vema.

Ingia katika furaha ya bwana wako

Tazama 25:19

Matthew 25:24

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kueleza mfano wa watumishi na talanta

Unachuma mahali ambapo hukupanda, na unavuna mahli ambapo hukupanda.

Maelezo haya mawili yanamaanisha kitu kilekile. Mtumwa anamlaumu bwana kwa kukusanya mazao ambayo siyo yake. "Unakusanya mazao ya bustani kutoka katika bustani ambazo huna haki ya kukusanya mazao hayo."

Kupanda

Siku hizo walizoea kutupa kiasi kidogo cha mbegu pande zote badala ya kupanda katika mistari.

Tazama, unapata ile ile ya kwako.

"Angalia, hii n"diyo yako"

Matthew 25:26

Sentensi unganishi

Yesu anaenedelea kueleza mfano wa watumishi na talanta.

Wewe mtumwa mwovu na mzembe.

"wewe ni mtumwa mwovu ambaye hutaki kufanya kazi."

Ninachuma mahali ambapo sikupanda na kuvuna mahali ambapo sikusiha.

Tazama 25:24

Kupokea tena ile yangu.

"Kupokea tena fedha yangu mwenyewe"

Faida.

Malipo yanayotolewa na benki kutokana na matumizi yasiyo ya kudumu ya pesa ya bwana.

Matthew 25:28

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kueleza mfano wa watumishi na talanta

mnyang'anyeni hiyo talanta

Bwana anawaambia wale watumishi wengine

talanta

Tazama 25:14

aliye na

"anayetumia vizuri alicho nacho"

ataongezewa zaidi

"Mungu atampa zaidi"

hata kwa kuzidishiwa

"hata zaidi"

kwa yeyote asiye na kitu

"Kwa yeyeote asiyetumia vizuri hicho alicho nacho.

Ambapo kutakuwa na kilio na kusaga meno

"Mahali ambapo watu watalia na kusaga meno yao."

"nacho atanyang'anywa"

nitakiondoa

mtupeni nje gizani huyo mtumishi asiyefaa, ambako kutakuwa na kilion a kusaga meno

"nje gizani ambako kuna kilio na kusaga meno"

Matthew 25:31

Sentensi unganishi

Yesu anaanza kuwaambia wanafunzi wake jinsi atakavyowahukumu watu atakaporudi wakatiwa mwisho

Mwana wa Adamu

Yesu anatumia nafsi ya tatu kuongea juu yake mwenyewe

Mataifa yote yatakusanyika mbele zake.

"Atayakusanya mataifa yote mbele zake."

Mbele zake.

"Mbele za uso wake."

Mataifa yote.

"Watu wote kutoka kila nchi."

kama vile mchungaji anavyotenganisha kondoo na mbuzi

Yesuanatumia msemo kuonesha jinsi atakavyowatenganisha watu

atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, bali mbuzi atawaweka mkono wake wa kushoto

atawaweka watu wenye haki upande wake wa kuume na atawaweka wenye dhambi upande wake wa kushoto

Matthew 25:34

Mfalme... mkono wake wa kulia

"Mimi mfalme, ... mkono wangu wa kulia"

Mfalme...mkono wake wa kulia

Yesu alijisema yeye mwenyewe katka nafsi ya tatu. AT: "Mimi, Mfalme...mkono wangu wa kulia."

Njoni, ninyi mliobarikiwa na Baba yangu.

"Njoni, ninyi ambao baba yangu amewabariki."

Baba yangu

Hili ni jina mashuhuri la Mungu linaloonesha uhusiano kati ya Mungu na Yesu

Urithini ufalme ulioandaliwa kwa ajili yenu.

"Urithini ufalme ambao Mungu ameufanya tayari kwa ajili yenu."

urithini ufalme ulioandaliwa kwa ajiloi yenu

"pokeeni baraka za utawala wa Mungu ambazo Mungu alipanga kuwapeni"

tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu

"Tangu hapo alipouumba ulimwengu"

Matthew 25:37

wenye haki

watu wenye haki

au kiu ... au uchi

"au ni lini tulipokuwa ukiwa na kiuau nilini tulipokuona u uchi"

Mfalme.

Hiki ni cheo kingine cha Mwana wa Mungu

na kuwaambia

"Akasema na wale walio mkono wa kulia."

Kweli nawaambia

"Nawaambia ukweli, "Huu ni msisitizo wa kile ambacho Yesu alikuja kusema baadaye"

kwa mmoja wa ndugu zangu wadogo

"mmoja wa wasio wa muhimu"

Ndugu zangu

"kaka zangu na dada" au "hawa ambao ni kama kaka zangu na dada zangu

mlinitendea mimi

"Ninajali kwamba mlifanya hivyo kwa ajili yangu."

Matthew 25:41

Ndipo atawaambia

"Ndipo mfalme atawaambia"

Mlio laaniwa.

"enyi watu ambao Mungu amewalaani."

Moto wa milele ambao umeandaliwa.

"Moto wa milele ambao Mungu ameandaa."

Malaika wake.

Wasaidizi wake.

Uchi lakini hamkunivika.

"Nilikuwa uchi lakini hamkunipa nguo."

Mgonjwa na niko kifungoni.

"Nilikuwa mgonjwa na nilikuwa kifungoni."

nikiwa mgonjwa na nikiwa kifungoni

"nilikuwa mgonjwa na nilikuwa gerezani"

Matthew 25:44

Sentensi unganishi

Yesu anahitimisha kuwaambia wanafunzi wake jinsi atakavyowahukumu watu atakapokuja mara ya pili

Maelezokwa ujumla

Huu ni mwisho wa sehemu ya habari inayoanzaia 23:1, mahali ambapo Yesu anafundisha juu ya wokovu na hukumu ya mwisho.

Wao pia watamjibu.

"Hao walioko kushoto pia watamjibu"

Mmoja wa wadogo hawa.

"Kwa yeyote kati ya watu wangu walio wadogo."

Hamkunitendea mimi.

"Nina jali kuwa hamkufanya kwa aajili yangu" au "Mimi ndiye hasa yule ambaye hamkumsaidia"

Hawa watakwenda katika adhabu ya milele

"Mfalme atawapeleka hawa kwenye eneo amablo watapata adhabu ambayo haitakoma"

Wenye haki kwenda katika uzima wa milele.

"Watu wenye haki wataenda katika uzima wa milele."

bali wenye haki katika uzima wa milele

"lakini mfalme atawapeleka hawa mahali ambapo wataishi milele pamoja na Mungu"

wenye haki

"watu wenye haki"

Matthew 26

Mathayo 26 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri zinaingiza nukuu kutoka kwa Agano la Kale. ULB inafanya hivyo kwa mistari iliyonukuliwa katika 26:31.

Dhana maalum katika sura hii

Kondoo

Hii ni taswira ya kawaida inayotumiwa katika Maandiko ya kutaja watu wa Israeli. Lakini, katika Mathayo 26:31, "kondoo" inawakilisha wanafunzi wa Yesu, ambao walikimbia wakati alikamatwa.

Pasaka

Kifo cha Yesu kilitokea kwa uhusiano na Sikukuu ya Pasaka kwa sababu yeye ndiye timizo la mwanakondoo wa Pasika. Ni kifo chake cha dhabihu ambacho kinatuokoa kutokana na hukumu ya Mungu.

Kula mwili na damu

Sherehe hii, ambayo mara nyingi huitwa "Meza ya Bwana," "Ekaristi", au "Ushirika Mtakatifu," hufanyika katika karibu makanisa yote hadi siku hii kwa ukumbusho wa dhabihu ya Kristo kwa ajili ya dhambi za binadamu. Hufanyika kwa kutii maagizo ya Yesu kwa wanafunzi wake katika Mathayo 26:26-28.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Aibu na woga

Kote katika sura hii, matendo ya viongozi wa Kiyahudi ni ya aibu na ya woga. Waliwaogopa watu waliopaswa kuwaongoza. Matendo yao ya aibu na ya uoga yanaweza kuwa vigumu kueleza katika kutafsiri.

Yuda kumbusu Yesu

Yuda amenakiliwa katika Mathayo 26:49 kumbusu Yesu ili kutoa ishara kwa askari ili kumtambua yule watakaomkamata. Miongoni mwa Wayahudi, kubusu ilikuwa njia ya kawaida ya kumsalimu mtu. Walikuwa na busu za aina mbalimbali kati ya watu wa tabaka mbalimbali. Kwa kuwa Yesu alikuwa mwalimu wa Yuda, labda alibusu mkono wake kama ishara ya heshima na utii.

"Haribu hekalu la Mungu"

Katika Mathayo 26:61, watu wawili wanamshtaki Yesu kwa kutaka hekalu la Yerusalemu liangamizwe ili aweze kulijenga kwa "siku tatu." Labda walikuwa wakimshtaki Yesu kwa kutukana hekalu na kwa hiyo, kwa njia nyingine, kumtukana Mungu. Mathayo hana rekodi ya Yesu akitamka haya, lakini maneno haya yapo katika Yohana 2:19.

Maneno "katika siku tatu" yanapaswa kueleweka kwa njia ya Kiyahudi kama "ndani ya siku tatu," wala sio "baada ya siku tatu."

<< | >>

Matthew 26:1

Maelezo kwa ujumla

Huu ni mwanzo wa sehehmu mpya wa simulizi amablao linaelezea kusulibiwa kwa Yesu, kufa na kufufuka. Hapa anawaeleza wanafunzi wake jinsi atakavyoteseka

Wakati Yesu alipomaliza

"kisha " au"baadaye"

Maneno haya yote.

Tazama 24:3

Mwana wa Adamu atatolewa ili asulibiwe.

"Baadhi ya watu watamtoa Mwana wa Adamu kwa watu wengine ambao watamsulibisha."

Mwana wa Adamu

Yesu anatumia nafsi ya tatu kuongea juu yake

Matthew 26:3

Sentensi unganishi

Mstari huu unatoa historia ya mpango wa viongozi wa Wayahudi wa kumkamata na kumwua Yesu

walikutana pamoja

"walikutana"

Kwa siri.

"Bila kujulikana kwa wengi"

Siyo wakati wa sikukuu.

"Tusimuue Yesu wakati wa sikukuu"

Sikukuu.

Sikukuu ya kila mwaka ya Pasaka.

Matthew 26:6

Sentensi unganishi

Hii inaanza na habari ya mwanamke akimwaga manukato ya gharama kabla ya kifo cha Yesu

Wakati

Hil ni neno linalotumika kuazisha habari mpya. Mathayo anaanza kuelezea habari mpya

Simoni mkoma

Inamaanisha kuwa huyu ndiye mtu ambaye Yesu alimponya kwa ukoma

Alipokuw amejinyoosha.

"Yesu alikuwa amekaa upande wake". Unaweza kutumia neno la lugha yako kwa mkao wa watu ambavyo huwa wakati wa kula.

Mwanamke alimwendea.

Mwanamke alikuja kwa Yesu.

Mkebe wa alabasta.

chombo ambacho hugharimu sana kwa kukinunua kilicho tengenezwa na jiwe laini.

Mafuta

Mafuta ambayo yana harufu nzuri.

aliyamimina juu ya kichwa chake

Yule mwanamke alifanya hivi kuonesha heshima kwa Yesu

Ni nini sababu ya hasara hii.

"Mwanamke huyu amefanya jambo baya kwa kuharibu mafuta haya"

Haya yangeweza kuuzwa kwa thamani kubwa na kupew masikini

"angweza kuyauza kwa thamani kubwa ya pesa na kuitoa ile pesa

kupewa masikini

"kwa watu masikini"

Matthew 26:10

Kwa nini mnamsumbua mwanamke huyu?

"Hamkupaswa kumsumbua mwnamke huyu"

kwa nini mna

viwakilishi vyote vya "mna" viko katika wingi

masikini

"watu masikini"

Matthew 26:12

mafuta

Tazama 26:6

kweli nawaambia

"nawambia ukweli" huu ni msisitizo wa kile kilichofuata

popote injili hii itakapohubiriwa

"popote pale watu watakapohubiri injili hii"

kitendo alichofanya huyu mwanamke, pia kitakuwa kinasemwa kwa ajili ya kumkumbuka

"watakumbuka kile ambacho mwanamke huyu amefanya na wataambiwa wengine juu yake"

Matthew 26:14

Sentensi unganishi

Yuda Iskaariote anakubali kuwasaidia viongozi wa Wayahudi kumkamata na kumwua Yesu

Nikimsaliti

"kuwasaidia kumkamata Yesu."

Vipande therathini vya fedha.

Kwa kuwa maneno haya ni sawa na yale ya unabii katika Agano la Kale, endeleza muundo huu badala ya kuugeuza katika pesa ya leo.

Kumsaliti kwao.

"Kuwasaidia wakuu wa makuhani kumkamata Yesu."

vipande thelathini

"vipande 30"

Matthew 26:17

Sentensi unganishi

Hii inaazisha hanari y a Yesu akisherehekea Pasaka pamoja na wanafunzi wake

Sasa

Hili ni neno amablo limetumika kuonesha mwazo wa habari mpya. Matahyo anaanza kueleza sehemu mpya ya habari

Alisema , "nendeni mjini kwa mtu fulani na mwambieni , 'Mwalimu anasema," Muda wangu umekaribia. Nitaitimiza Pasaka pamoja na wanafunzi wangu katika nyumba yako."''

"Aliwaambia wanafunzi wake kuingia mjini kwa mtu fulani na kumwambia kwamba Mwalimu anamwambia, 'Muda wangu umekaribia. Nitaitimiza Pasaka pamoja na wanafunzi wangu nyumbani mwako.'" au "Aliwaambia wanafunzi wake kwenda mjini kwa mtu fulani na kumweleza mtu huyo kwamba Mwalimu anasema muda wake umekaribia na atatimiza Pasaka pamoja na wanafunzi wake katika nyumba ya mtu huyo."

Muda wangu.

Maana yake yaweza kuwa: 1) " Muda ambao niliwahi kuwajulisha" au 2 "Muda ambao Mungu amepanga kwa ajili yangu."

Umekaribia.

Maana yake yaweza kuwa: 1) "uko karibu" au 2) "Umefika."

Timiza Pasaka.

"Kula chakula cha Pasaka" au "sherekea sikukuu ya Pasaka kwa kula chakula maalum."

Matthew 26:20

Aliketi chini apate kula.

Tumia neno kwa mkao ambao watu katika utamaduni wako daima hukaa wakati wa kula.

kweli nawaambia

"Nawaambia ukweli." Huu ni msisitizo wa kile kilichofuata

Hakika siyo mimi, Bwana?

"Nina hakika mimi siye, Je, ni mimi?"

Matthew 26:23

Mwana wa Adamu

Yesu anatumia nafsi ya tatu kuongea juu y ake mwenyewe

ataondoka

"akufa"

kama ilivyoandikwa

"kama vile manabii walivyoandika juu yake katika maandiko"

Mtu yule ambaye kwake Mwana wa Adamu asalitiwa.

"Mtu ambaye amsaliti Mwana wa Adamu."

Je, ni mimi Tabi?

"Rabi, kwa hakika si mimi nitakayekusaliti"

Umesema jambo hilo wewe mwenyewe

"wewe ndiye unayesema"

Matthew 26:26

Sentensi unganishi

Yesu anakula chakula na wanafunzi kwa kusherehekea Pasaka na wanafunzi wake

Alichukua... alibariki.

Tazama 14:19

Matthew 26:27

kutwaa au chukua.

Tazama14:19

kikombe

Kikombe kinamaanisha kikombe kikiwa na divai ndani yake

kunyweni

"kunywa divai kutoka kikombe hiki"

kwa kuwa hii ni damu yangu

"kwa kuwa hii divai ni damu yangu"

Damu ya agano.

"Damu ambayo huonesha kwamba agano linafanya kazi" au "damu ambayo hufanya agano liwezekane.

Inamwagwa.

"Inamwagwa kwa ajili ya kifo" au "hivi punde itachuruzika kutoka mwilini mwangu." au "itachuruzika kutoka katika majeraha yangu nitakapo kufa."

matunda ya mzabibu.

"mvinyo"

Lakini nawaambia

Hii inaongeza msisitzo

katika Ufalme wa Baba yangu.

Baba atakapoanzisha ufalme wake duniani "hapa"

wa baba yangu

Hiki ni cheo muhimu cha Mungu kinachoonesha uhusiano muhimu kati ya Mungu na Yesu.

Matthew 26:30

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwafundisha wanafunzi wake wakati wakielekea mlima wa Mizeituni

Maelezo kwa ujumla

Katika mstari wa 31, Yesu anamnukuu Nabii Zekaria kuonesha kuwa ili kutimiza unabii, wanaaafunzi wake wataondoka.

Wimbo.

Wimbo wa sifa kwa Mungu.

kujikwaa

"mtaniacha"

Kukataa.

"Kuniacha."

kwa kuwa imeandikwa

Kwa kuwa nabii zekaria aliandika tangu awali katika maandiko"

Nitampiga

kiwakilishi "ni" kinamaanisha Mungu. Inamaanisha kuwa Mungu atasababisha au kuruhusu watu kumwumiza na kumwua Yesu

mchungaji ... na kondoo wa kundi

Yesu na wanafunziwake

Kondoo wa kundi watatawanyika

"Watawatawanya kondoo wote wa kundi"

Baada ya kufufuka kwangu

"Baada ya Mungu kunifufua"

Matthew 26:33

Kukataa.

Tazama 26:30

kweli nakuambia

"Ninakuambia ukweli" Hiiinaongeza msisitizo wa kile kilichofuata baadaye

Kabla jogoo hajawika.

"Kabla jua halijachomoza."

Jogoo.

Ndege ambaye huwika kwa sauti kubwa karibu na majira ya jua kuchomoza.

Kuwika.

Sauti ambayo jogoo hufanya anapowika.

utanikana mara tatu

"utasema mara tatu kuwa wewe si mfuasi wangu"

Matthew 26:36

Sentensi unganishi

Hii inaazisha habariy a Yesu akiomba Gethsemane

na akaanza kuhuzuniaka

"na akawa na huzuni sana"

Roho yangu inahuzuni kubwa sana

Hapa roho inamaanisha nafsi nzima ya mtu. "Nina huzuni sana"

kiasi cha kufa

"Najihisi kama nataka kufa"

Matthew 26:39

Alianguka kifudifudi.

Kwa makusudi kuweka uso chini ili upate kuomba.

Baba yangu.

Hili ni jina maarufu la Mungu ambalo huonesha uhusiano kati ya Mungu na Yesu.

KIkombe hiki kiniepuke.

Usemi huu, "kikombe hiki" huashiria mateso ambayo Yesu atapitia.

Hata hivyo, siyo kama nipendavyo, bali kama utakavyo.

Hii inaweza kuelezwa kama sentensi iliyo kamilika. "Lakini usifanye kile nitakacho bali kile utakacho."

akamwambia Petro, kwa nini hamkukesha

Yesu anamwambia Petro, kiwakilishai cha "hamku" ni cha wingi kinamaanisha Petro, Yakobo na Yohana.

kwa nini hamkuweza kukesha nami hata kwa saa moja?

"Ninasikitaka kuwa hamkuweza kukesha nami hata kwa saa moja"

msiingie katika majaribuni

"mtu yeyote asiwajaribu mtende dhambi"

Roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu

Roho inamaanishahamu ya nafsi. Na "mwili" inamaanisha mwanadamu kamili. Yesu anamaanisha wanaweza kuwa na hamu ya kufanya mapenzi ya Mungu, Lakini kama wanadamu ni wadhaifu na wanaweza kushindwa

Matthew 26:42

Akaenda zake.

"Yesu alienda zake."

mara ya pili ... mara ya tatu

mpangilio kwa nafasi za namba

Nisipokinywea.

"Isipokuwa kukinywea kikombe hiki cha mateso."

Baba yangu.

Hili ni jina mashuhuri la Mungu ambalo hueleza uhusiano kati ya Mungu na Yesu.

Macho yao yalikuwa mazito.

"Walikuwa wakisinzia- sinzia sana."

hili haliwezi kuepukika

"lazima nikinywee"

kama jambo hili

J"ambo hili" inamaanisha kikombe na kile kilichomo.

na ni lazima nikinywee

"lazima nikinywee" lazima nikinywee kikombe cha mateso"

mapenzi yako yatimizwe

"kile utakacho kifanyike"

macho yako yalikuwa mazito

"walikuwa na usingizi mzito"

Matthew 26:45

Bado mmelala tu na kijipumzisha

Ninasikitika kwamba bado mmelala na kupumzika"

Saa imekaribia.

"Muda umefika."

na Mwana wa Adamu anasalitiwa

"kuna mmoja wenu anamsaliti mwana wa Aadamu"

Mikono ya wenye dhambi.

Neno "mikono" linamaanisha mamlaka ya kutawala. "Watu wenye dhambi."

Tazameni

"Zingatia kile ambacho nataka kuwaambia."

Matthew 26:47

Sentensi unganishi

Hii inaazisha habari ya Yuda wakati alipomsaliti Yesu na viongozi wa dini wakamkamata

Wakati alipokuwa bado akiongea.

"Wakati Yesu alipokuwa bado akiongea."

marungu

vipande vikubwa vya miti vya kupigia watu

Sasa ... mkamateni

Neno "sasa" linaonesha kuanza kwa habari mpya. Mathayo anaeleza jinsi Yuda atakavyotoa ishara atakayotoa kwa nia ya kumsaliti.

Akisema, "Yule nitakaye mbusu, ndiye yeye. Mkamateni."

"Akasema kwamba yule aliye mbusu ndiye waliyepaswa kumkamata."

Huyo nitakaye mbusu.

"Yule nitakaye mbusu" au "Mtu ambaye nita mbusu."

Busu.

Namna ya heshima ya kumsalimia mwalimu wa mtu mwingine.

Matthew 26:49

alikuja kwaYesu.

"Yuda alimtokea Yesu."

Alimbusu.

"Akakutana naye kwa kumbusu."

ndipo wakaja

"Kiwakilishi "waka.." kinamaanisha wale watu waliokuja na Yuda wakiwaa na marungu na mapanga pamoja na viongozi wa dini

Wakamnyooshea Yesu mikono.

Wakamkamata Yesu"

Matthew 26:51

Tazama.

Neno "tazama" linatuvuta usikivu kwa ajili ya taarifa ya kugusa inayofuatia.

alichomoa upanga

"aliyechukua upanga ili aue wengine"

wataangamizwa kwa upanga

"watakufa kwa njia ya upanga" au "mtu atawaua kwa upanga"

Mnadhani kuwa siwezi kumwita Baba, na angenitumia zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika?

"Mlipaswa kujua kwamba ningeweza kumwita Baba yangu, na angenitumia majeshi zaidi ya kumi na mawili ya malaika."

mnadhani

hapa "mna" neno la umoja linlomaanisha yule mtu aliye na upanaga.

Baba yangu.

Hili ni jina mashuhuri la Mungu ambalo hueleza uhusiano kati ya Mungu na Yesu.

Majeshi ya malaika zaidi ya kumi na mawili.

Neno "jeshi" ni neno la kijeshi linalojumuisha wanajeshi 6,000. Yesu anamaanisha kuwa Mungu angeweza kutuma malaika wa kutosha kuwazuia wale waliokuwa wanamkamata. Zaidi ya makundi 12 ya malaika.

lakini bai jinsi gani maandiko yangeweza kutimizwa, hivi ndivyo ilipswa kutoka

"Lakini kama nkifanya hivyo, nisingeweza kutimiza,kile Mungu alichosema kwenye maandiko kitokee"

Matthew 26:55

Je, mmekuja na mapanga na marungu kunikamata kama mnyang'anyi?

"Mnajua kwamba mimi siyo mnyang'anyi, hivyo ni makosa yenu kuniijia mkiwa na mapanga na marungu.

Marungu.

Vipande vikubwa vya miti migumu kwa ajili ya kupigia watu.hekaluni

hekaluni

Inaoneshakuwa Yesu hakuwa hekaluni. alikuwa kwenye korido la hekalu

ili maandiko ya manabii yatimie

"napenda kutimiza kile ambacho manabii waliandika kwenye maandiko"

Kumuacha.

Kujitenga naye au walijitenga naye.

Matthew 26:57

Sentensi unganishi

Hii inaanzisha habari ya majaribu ya Yesu kwenye baraza la viongozi wa dini ya Wayahudi

Petro alimfuata

"Petro alimfuata Yesu

Ukumbi wa Kuhani Mkuu.

Sehemu ya uwazi karibu na nyumba ya Kuhani Mkuu.

Aliingia ndani

"Petro aliingia ndani"

Matthew 26:59

Sasa

Hili neno linaonesha kuazisha habari mpya kwenye simulizi. Matahyo anaanza kueleza habari mpya ya simulizi

kusudi wapate

kiwakilisi "wa" kinamaanisha wale wakuu wa Makuhani na wale wajumbe wa baraza.

Wawili walitokeza mbele.

"Wanaume wawili walikuja mbele" au "mashahidi wawili walitokeza mbele."

Walisema, "Mtu huyu alisema, 'Ninaweza kuliharibu hekalu la Mungu na kulijenga upya kwa siku tatu.'"

"Walishuhudia kwamba walimsikia Yesu akisema angeweza kuvunja hekalu la Mungu na kulijenga upya kwa muda wa siku tatu."

Mtu huyu alisema.

"Mtu huyu Yesu alisema."

Matthew 26:62

hawa wanakushuhudia nini dhidi yako?

"unajibu nini juu ya ushuhuda huu dhidi yako?"

Mwana wa Mungu.

Hili ni jina mashuhuri ambalo hueleza uhusiano kati ya Kristo na Mungu.

Mungu aishivyo

Tazama 16:13

Umesema jambo hilo wewe mwenyewe.

Yesu anathibitisha kwamba yeye "ndiye Kristo, Mwana wa Mungu. "Kama ulivyosema, Mimi ndiye" au "Umekubaliana na ukweli huo"

Lakini nakuambia, tangu sasa na kuendelea

Neno "wewe" ni la wingi. Yesu anamwambia kuhani mkuu na kwa wengine waliokuwapo hapo.

Tangu sasa na kuendelea mtamwona Mwana wa Adamu.

Maana zinaweza kuwa: 1) Watamuona Mwana wa Adamu baadaye kwa wakati ujao au 2) kwa "sasa" Yesu anamaanisha wakati wa kifo chake, kule kurudi kwake kutoka kwa wafu, na kupaa kwake kwenda mbinguni.

Mwana wa Adamu

Yesu anatumia nafsi ya tatu kuongea juu yake

Upande wa mkono wa kulia wenye nguvu.

"Upande wa mkono wa kulia wa Mungu mwenyezi"

Akija katika mawingu ya mbinguni.

"Akisafiri kuja duniani katika mawingu ya mbinguni."

Matthew 26:65

Kuhani Mkuu alirarua mavazi yake.

Kuchana mavazi ilikuwa ni ishara ya huzuni na hasira.

amekufuru

kwa kufuru hii, inamaanisha kuwa Yesu alikuwa akidai kuwa yeye ni sawa na Mungu

Je, twahitaji tena ushahidi?

"hatuhitaji kusikia ushahidi mwingine"

Tayari mmesikia

kiwakilishi cha "mme" kikokatika wingi kinamaanisha wajumbe wa baraza.

Matthew 26:67

Kisha wali

Maana yaweza kuwa: "Kisha baadhi ya watu" au "Kisha askari"

Walimtemea usoni.

Hili ni tendo la kufedhehesha.

Tutabirie.

Hapa "tutabirie" humaanisha, "tuambie kwa kutumia uwezo wa Mungu." Haimaanishi, "tuambie kitu gani kitatokea kwa wakati ujao."

Wewe Kristo

Wale waliokuwa wakimpiga Yesu. Walimwita kwa kumdhihaki

Matthew 26:69

Sentensi unganishi

Hii ni habri ya Petro akimkana mara tatu kuwa anamjua Yesu, kama vile Yesu alivypkuwa amaesema kuwa atafanya.

Maelezo kwa ujumla

Matukio haya yanatokea sambamba na majaribu ya Yesu kwa viongozi wa dini

Wakati huo

Hili neno linaonesha kuanza kwa habari nyingine. Mathayo anaanza kuwaambia sehemu ya habari.

Sijui kile unachosema.

Petro aliweza kufahamu alichosema mjakazi. Alitumia maneno haya kukana kwamba alikuwa pamoja na Yesu.

Matthew 26:71

Alipo...

"Petro alipo..."

Lango.

Uwazi katika ukuta kwenye ukumbi.

Akakana tena kwa kiapo, "mimi sim"jui mtu huyu

"akakana tena na kusema, 'Naapa simjui mtu huyu'"

Matthew 26:73

Mmoja wao.

"Mmoja wa hao waliokuwa pamoja na Yesu."

Kwa kuwa rafudhi yako huonesha.

"Tunaweza kukuambia kwamba unatoka Galilaya kwa sababu unaongea kama Mgalilaya."

kulaani.

"Kujitakia laana iwe juu yake mwenyewe."

jogoo akawika

Tazama 26:33

Petro alikumbuka maneno aliyoambiwa na Yesu, "kabla jogoo hajawika utanikana mara tatu."

Ptro alikumbuka kuwa Yesu alikuwa amemwambia kuwa kabla jogoo hajawika atakuwa amemkana mara tatu"

Matthew 27

Mathayo 27 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

"Walimpeleka kwa gavana Pilato"

Wayahudi walikuwa chini ya utawala wa Ufalme wa Kirumi, na Warumi hawakuwaruhusu watoe uhai wa mhalifu yeyote bila kupata ruhusa kwanza. Kwa hivyo viongozi wa Kiyahudi walimuomba Pontio Pilato athibitishe hukumu yao juu ya Yesu. Pilato alijaribu kuepuka kuthibitisha uamuzi wao. Alijaribu kuwafanya viongozi wa Kiyahudi kuchagua kati ya kumkomboa Yesu au mfungwa mbaya sana aliyeitwa Baraba.

Kaburi

Kaburi ambamo Yesu alizikwa (tazama: Mathayo 27:59-60) ilikuwa ni aina ya kaburi ambamo Wayahudi tajiri walizikwa. Ilikuwa na chumba halisi ambacho kilichombwa kwenye mwamba, ambapo miili ilikuwa imefungwa na kuwekwa kwenye miamba ilivyokuwa kwenye kuta. Baadaye, wakati miili imeharibika na kubakia mifupa iliyo wazi, mifupa hiyo ilikusanywa na kuingizwa kwenye mitungi maalum inayoitwa mabasi. Makaburi hayo yalifungwa na mwamba mmoja mkubwa wa kutosha kuufunga mlango. Mwamba huu ulikuwa umevingirwa au kuwekwa mahali pa mlango mwa kaburi.

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

"Shikamoo, Mfalme wa Wayahudi!"

Kifungu hiki, kinachopatikana katika Mathayo 27:29, ni mfano wa kinaya. Katika takwimu hii ya matamshi, kitu kinasemwa ili kuashiria kitu kingine, mara nyingi maana yake ikiwa ni kinyume. Tamko "Shikamoo" ilikuwa salamu iliyotumiwa na watu nyakati maalum, mara nyingi mbele ya wafalme na malkia. Hata hivyo, askari waliomdhihaki Yesu hawakutaka kumheshimu. (Angalia: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-irony)

<< | >>

Matthew 27:1

Sentensi unganishi

Hii inaanzisha kujariwa kwa Yesu mbele ya Pilato

Muda wa asubuhi

neno linamaanisha kuazisha habari mpyakataika simulizi. Matahyo anaanza kueleza habari mpya katika sehemu hii

walikula njama dhidi ya Yesu wapate kumuua

Viongozi wa Wayahudi walikuwa wakipanga jinsi ya kuwashawishi viongozi wa Rumi jinsi ya kumuua Yesu

walimwongoza

"walimkabidhi" au "walimpeleka"

Matthew 27:3

Sentensi unganishi

Mwanadishi amekoma kueleza habari ya kuhojiwa kwa Yesu na anaeleza jinsi Yuda alivyojiua

Maelezo kwa ujumla

Tukio hili limeanza baada ya Yesu kuhojiwa mbele ya baraza la viongozi wa Wayahudi, lakinni hatujui kama hii ilitokea baada au kabla ya mahojiano ya Yesu kwa Pilato

Kisha wakati Yuda

Kama lugha yako ina namna ya kuonesha habari mpya inapoanza, unaweza kuitumia hapa.

Yesu amaekwisha kuhukumiwa

"Viongozi wa Wayahudi wameshamhukumu Yesu"

vipande thelathini vya fedha

Tazam 26:14

damu isiyo na hatia

"mtu ambaye hakustahili kufa"

inatuhusu nini?

"hilo siyo tatizo letu" au "hilo ni tatizo lako"

alivirusha chini vile vipande vya fedha katika hekalu"

Hii inamaanisha 1) alivitupa vile vipande vya fedha akiwa kwenye korido la hekalu, au 2) alikuwa amesimama kwenye korido la hekalu na akavitupa vile vipande vya fedha hekaluni.

Matthew 27:6

si halali kuiweka fedha hii

"Sheria zetu hazituruhusu kuiweka hii"

Kuiweka hii

"kuiweka fedha hii"

hazina

ahaili ni eneo ambalo waliweka ile fedha waliyotumia kwa mahitaji ya hekaluni nakwa makuhani.

gharama ya damu

Hii ni nahau inayomaanisha pesa i;iyotumika kumlipa mtu aliyeua mtu. "Pesa iliyolipwa kwa ajili ya kuuawa kwa mtu"

shamba la mfinyanzi

Hili n ishamba ambalo lilikuwa limenunuliwa kwa ajili ya kuwazikia wageni waliofia Yerusalemu

hilo shamba limekuwa likiitwa

"watu huliita shamba hilo"

hadi leo hii

Hadi wakati ambao Mathayo alikuwa anaandika kitabu hiki.

Matthew 27:9

Maelezo kwa ujumla

Mwandishi ananukuu toka maandiko ya Agano Jipya kuonesha kuwa kujinyonga kwa Yuda kulikuwa kutimiza unabii

Kisha lile neno lililokuwa limenwa na nabii Yeremia litimie

"Hili liltimiza unabii ambao nabii Yeremia alisema"

gharama iliyopngwa na watu wa Israel

"Gharama ambayo watu wa Isrel walimpngia"

watu wa Israel

Hii inamaanisha baadhi ya watu wa Isrel waliolipa ili Yesu auawe. "baadhi ya watu wa Israel" au "viongozi wa Israel"

alivyokuwa amenielekeza

kiwakilishi "ni" kinamaanisha Yeremia

Matthew 27:11

Senteni unganishi

Ni habari inayoanzi 27:1

Sasa

Kama lugha yako ina maneno yanyotumika kuendeleza mazungumzo baada ya pumziko la hadithi kubwa, waweza kuyatumia hapa

liwali

"Pilato"

wewe wasema hivyo

Hii ni nahau ambayo Yesu anatumia kumaanisha "ndiyo" lenye lengo lakumaanisha kutoweka wazi alichokuwa anasema "wewe ndiye unayesema" au "unaonesha kukiri"

wakati aliposhitakiwa na wakuu wa Makuhani na wazee

"Lakini wakati wakuu wa makuhani na wazee walipomshitaki"

Hyasikii mashaitaka yote dhidi yako?

Pilatoanauliza swali kwa sababu anashangazwa na ukimya wa Yewsu. "Ninashangazwa kwamba huwajibu hawa watu wanokushitaki kwa kutenda mabaya"

neno moja, hivyo liwali alijawa na mshangao

"neno moja; hii ilimshangaza sana liwali"

Matthew 27:15

Sasa

Hili ni neno linalotumika kuosha mwanzo wa habari kuu ili kwamba mwandishi aweze kutoa taarifa za kumsaidia msomaji kinachotokea kuanzia 27:17

Sikukuu

Hii ni sikuu ya kusherehekea Pasaka

mfungw mmoja anayechaguliwa na umati

"mfungwa ambaye umati utamchagua"

walikuwa na mfungwa sugu

"kulikuwa na funwa sugu"

sugu

anayejulikan vizuri kwa kutenda makosa makubwa

Matthew 27:17

walipokiuwa wamekusanyika

"umati ulikuwa umekusanyika"

Yesu anayeitwa Kristo

ambaye watu baadhi humwita Kristo

wamekwisha kumkamata Yesu

viongozi wa Wayahudi walikuwa wamemleta Yesu kwake. "walifanya haya ili kwamba Pilato amhukumu Yesu.

alipokuwa akiketi

"Pilato alopokuwa ameketi"

alipokuwa akiketi kwenye kti chake cha hukumu"

"Kuketi kwenye kiti cha hakimu." Hapa ndipo hakimu huketi anapokuwa akifanya maamuzi.

alimtumia neno

"neno" inamaanisha ujumbe. "alituma ujumbe"

leo nimeteswa mno

"Nimeteseka san leo"

Matthew 27:20

Ndipo ... Yesu auawe

Neno "ndipo" limetumika kumaanisha mwanzo wa habari. Yesu anaeleza kwa nini umati ulimchagua Baraba.

Yesu auawe

Askari wa Rumi wamuue Yesu"

aliwauliza

"aliuliza umati"

anayeitwa Kristo

"ambaye watu baadhi humwita Kristo"

Matthew 27:23

ametenda

"ambalo Yesu ametenda"

walipaza sauti

"walipiga kelele"

akanawa mikono yake mbele ya umati

Pilato alifanya hivi kama ishara ya kuwa yeye hawajibiki kwa kifo cha Yesu

damu

"damu" inamaanisha damu ya mtu "kifo"

yaangalieni haya wenyewe

"huu ni wajibu wenu"

Matthew 27:25

Damu yake iwe juu yetu na watoto wetu

damu inamaanisha kifo cha mtu. Kirqai cha "iwe juu yetu na watoto wetu" ni nahau inayomaanisha kuwa wanakubali kuajibika kwa kile kinachotokea. "Ndiyo! Sisi na wa watoto wetu tutaajibika kwa kifo cha Yesu"

alimpiga mijeredi

Maaskari wa Pilato walimpiga mijeredi Yesu.

kupiga mijeredi

kumpiga mtu kwa kutumia mjeredi

Kumkabidhi kwao kwenda kusulibiwa

"na Pilato akaamuru Yesu asulibiwe"

Matthew 27:27

Sentensi unganishi

Hii inaanzisha habari ya kusulibiwa kwa Yesu

kundi kubwa la maaskari

"kikosi cha maaskari

wakamvua

"kumvulisha nguo"

nyekundu

"nyekundu yenye mng'ao

taji ya miiba

"taji iliyotengenezwa kwa matawi ya miiba" au "taji ilitengenezwa ka matawi yalyo na miiba"

mwanzi katika mkono wake wa kuume

Walimpa Yesu ashikilie fimbo kuonesha kuwa wafalme hushilia fimboya enzi. walifanya hivi kumkejeli.

salalmu mfalme wa Wayahudi

walisema hivi kumkejeliYesu. walikuwa wakimwita Yesu "mfalme, wa Wayahudi," lakini kwa hakika hawakuamini kuwa Yesu alikuwa mfalme. Lakini walichokuwa wakisema kilikuwa kweli.

Matthew 27:30

walimtemea mate

"maaskari walimtemea Yesu"

Matthew 27:32

Walipotoka nje

Hii inamaanisha Yesu na maaskari walitoka nje ya mji, "walipokuwa wakitoka nje ya Yerusalaem"

walimwonamtu

"maaskari walimwona mtu"

ambaye walimulazimisha kwenda nao ili apate kubeba msalaba wake

"amabye maaskari walimlazimisha kwenda naye ili kwamba abebe msalaba wa Yesu"

mahali paitwapo fuvu la kichwa

"eneo ambalo watu waliliita Golgotha"

Walimpa siki iliyochanganywa na nyongo.

"walimpa siki, ambayo walikuwa wameichanganya na nyongo"

siki

kinwaji kichungu cha njano ambacho miili hukitumia kwa mmeng'enyo wa chakula

Matthew 27:35

mavazi

Hili ni vazi ambalo Yesu alikuwa akilivaa

Juu ya kichwa chake waliweka mashitaka dhidi yake

"mashitaka" inamaanisha waliandika ili kuonesha sababu za kumsulibisha Yesu

Matthew 27:38

wanyang'anyi wawili walisulibishwa pamoja naye

Maskari walimsulibishaYesu pamoja na wanyanga'nyi wawili

wakitikisa vichwa vyao

walifanya hivi kumcheka Yesu

Kama nia mwana wa Mungu shuka chini

Kama wewe ni mwana wa Mungu thibitisha kwa "kushuka msalabani"

Mwana wa Mungu

Hiki ni cheo cha muhimu amabcho kinaonesha uhusiano kati ya Kristo na Mwanawa Mungu

Matthew 27:41

Aliokoa wengine, lakini hawezi kujiokoa mwenyewe

Maana yake yaweza kuwa 1) viongozi wa Wayahudi hawakuamini kuwa Yesu aliwaokoa wengine au kwamba anaweza kujiokoa wenyewe au 2) waliamini kuwa Yesu aliwaokoa wengine na sasa wanamcheka kwa sababu sasa hawezi kujiokoa mwenyewe

yeye ni mfalme

Viongozi wanamkejeli Yesu. Wanamwita "Mfalme wa Israel," Lakini kwa uhalisia hawaamini kuwa yeye ni Mfalme. "Anasema kuwa yeye ni mfalme wa Israel"

Matthew 27:43

Sentensi unganishi

Viongozi wa Wayahudi wanaendelea kumkejeli Yesu

Kwa sababu alisema, 'Mimi ni Mwana wa Mungu.'

"Kwa sababu Yesu alisema kuwa yeye ni Mwana wa Mungu"

Mwana wa Mungu

Hiki ni cheo cha maalumu cha Yesu ambacho kinaelezea uhusiano na Mungu

Na wale wanyang.nyi waliokuwa wamesulibiwa pamoja naye

"Na wale wanyanga'nyi ambao maaskari waliwasulibisha pamoja na Yesu"

Matthew 27:45

Sasa

Neno hili limetumika kuonesha kuanza kwa habari nyingine. Mathayo anaanza kueleza sehemu mpya ya habari

kutoka saa ya sita ... hadi saa tisa

Kuanzia mnamo adhuhuri ... kwa muda wa saa tatu" au "kuazia mnamo muda wa saa sita mchana ... hadi mnamo muda wa saa tisa mchana"

kulikuwa na giza katika nchi yote

Neno "giza" ni nomino. "ilikuwa giza nchi yote"

Yesu akalia

"Yesu akaita" au "Yesu alipiga kelele"

Eloi. Eloi. lamathabakithani

Haya ndiyo maneno amabyo Yesu aliita kwa sauti kuu katika lugha ya.ke

Matthew 27:48

mmoja wao

inaweza kumaanisha 1)mmoja wa maaskari au 2) mmoja wale waliokuwa wamesimama karibu wakitazama

sifingo

Huyu ni mnyama wa majini ambaye anapokuwa amevuliwa lile ganda lake liliweza kutumika kwa kuwekea vitu kama maji na kinywaji ambacho kinaweza kusukumwa nje.

na kumpa

"akampa Yeu

akaitoa nafsi yake

"akafa akiitoa roho yake kwa Mungu" au "akapumua pumzi ya mwisho"

Matthew 27:51

Sentensi unganishi

Hii inaanza na matukio ambayo yalitokea baada ya Yesu kufa

Tazama

Neno "tazama" linatutaka kuwa makini kwa taarifa za kushangaza zinazofuata.

pazia la hekalu lilipasuka

"lile pazia la hekaluni lilipasuka katika sehamu mbili" au "Mungu alilifanya pazia la hekalu ligawanyike mara mbili"

Makaburi yalifunguka, na miili ya watakatifu wengi waliokuwa wamelala usingizi walifufuliwa.

"Mungu alifunua makaburi na kuifufua miili ya watu wengi wa Mungu waliokuwa wamekufa"

wamelala usingizi

Hii ni tafsida yenye maana ya kufa "waliokuwa wamekufa"

Makaburiyalifunuka ... na walionekana kwa wengi

Mpangilio wa matukio haya hauko wazi sana. Baada ya tetemeko la ardhi wakati Yesu alipokufa na makaburi kufunuka 1)Watu watakatifu walikuwa hai tena, kisha baada ya Yesu kufufuka, watakatifu wakauingi mji wa Yerusalemu na watu wengi waliwaona, au 2)Yesu alifufuka, kisha watakatifu nao wakafufuka na kuuingia mji ambapo watu wengi waliwaona.

Matthew 27:54

Basi

Hili neno limetumika kuonesha mwanzo wa habari mpya. Mathayo anaaza kueleza sehemu nyingine ya habari

na wale ambao walikuwa wakimtazama

"na wale maaskari waliokuwa wakimtazama Yesu"

Mwana waMungu

Hiki ni cheo maalumucha Yesu kinachoonesh uhusiano na Mungu

mama wa watoto wa Zebedayo

"Mama wa Yohana na Yakobo" au "mke wa Zebedayo"

Matthew 27:57

Sentensi unganishi

Hii inaanza na habari ya kuzikwa Kwa Yessu

Arimathayo

Hili jina la mji ulioko Israel

Pilato aliagiza apate kupewa

"Pilato aliwaagiza maaskari kumpa Yusufu mwili wa Yesu"

Matthew 27:59

sufi safi

Nguo laini ya thamani

aliliokuwa amelichonga mwambani

Inamaanisha kuwa Yusufu aliajiri watu ambao waliochonga hilo akaburi

akavingirisha jiwe kubwa

Yawekana Yusufu alikuwa na watu wengine pale waliomsaidia kulivingirisha lile jiwe

kuelekea kaburi

"karibu na kaburi"

Matthew 27:62

maandalio

Hii ni siku ambayyo watu waliandaa mabo yao kwa sababu ya sabato

walikusanyika pamoja kwaPilato

"walikutana na Pilato"

yule mdanganyifu alipokuwa hai

"wakati mdanganyifuYesu alipokuwa hai"

alisema, 'baada ya siku tatu atafufuka tena.'

"alisema kwamba baada ya siku tatu atafufuka tena"

agiza kwamba kaburi lilindwe salama

"waagize maaskari wako kulilinda kaburi"

siku ya tatu

siku ya 3

kumuiba

"kuiba mwili wake"

na kusema kwa watu, 'Amefufuka kutoka wafu.'

"na kuwaambia watu kwamba amefufuka kutoka wafu"

Na udanganyifu wa mwisho utakuwa mbaya kuliko wa kwanza

"kama watawadanganya watu kwa kusema hivyo, itakuwa vibaya kuliko alivyowadanganya watu kwa kusema kuwa yeye ni Kristo"

Matthew 27:65

walinzi

kwa Warumi Ilimaanisha maaskari wanne hadi kumi na sita

jiwe liligongwa muhuri

Inaweza kumaanisha 1) waliweka kamba karibu na jiwe na kuliunganishana kuta za lile jiwe katika pande zote za lango la kaburi au 2) waliweka mihuri katkati ya jiwe na kuta

na kuweka walinzi

"kuwaambia walinzi wasimame mahali ambapo wataweza kuwazuia watu ambao watadirika kufanya chochote kaburini.

Matthew 28

Mathayo 28 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

"Wafanye wanafunzi"

Aya mbili za mwisho (Mathayo 28:19-20) zinajulikana kama "Tume Kubwa" kwa sababu zina amri muhimu sana iliyotolewa kwa Wakristo wote. Wakristo wanapaswa "wafanye wanafunzi" kwa kwenda kwa watu, kuwapa injili na kuwafundisha kuishi kama Wakristo.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Malaika wa Bwana

Mathayo, Marko, Luka, na Yohana wote waliandika juu ya malaika waliovalia nguo nyeupe wakiwa pamoja na wanawake kwa kaburi la Yesu. Waandishi wawili kati yao waliwaita wanaume, lakini ni kwa sababu tu malaika walikuwa katika hali ya kibinadamu. Waandishi wawili waliandika kuhusu malaika wawili, lakini waandishi wengine wawili waliandika juu ya moja tu. Ni bora kutafsiri kila moja ya vifungu hivi kama inavyoonekana katika ULB bila kujaribu kufanya vifungu vyote kufanana. (Angalia: Mathayo 28:1-2, Marko 16: 5 na Luka 24: 4 na Yohana 20:12)

__<< | __

Matthew 28:1

Sentensi ungsnishi

Hii ni habari ya ufufuo wa Yesu kutoka wafu

Baadye jioni siku ya Sabato, jua lilipokuwa likichwa kuelekea siku ya kwanza ya juma

Baada ya Sabato kuisha, jua lilipokuwa likichomoza Jumapili asubuhi"

Baadaye

Hili ni nenolinaloonesha kuanza kwa habari mpya. Mathayo anaanza kueleza sehemu mpya ya habari hii

Mariamu mwingine

Huyu ni Mariamu mama wa Yakobo na Yusufu Tazma (27:54)

Tazama

Neno "tazama" linatutahadharisha kuwa tayari kwa ajili ya taarifa kushanagaza ambazo zinafuata. Lugha yako inaweza kuwa namna ya kulisema hili.

kulikuwa na tetemeko kubwa, kwa sabau malaika wa Bwana alishuka ... na kulivingirisha jiwe

Yaweza kumaanisha yafatayo 1) tetemeko lilitokea kwa sababu alishuka na kulivingirisha lile jiwe au 2) matukio yote haya yalitokea kwa wakati mmoja.

tetemeko

kutetemeka ghafla kwa ardhi

Matthew 28:3

Sura yake

"Sura ya malaika"

ilikuwa kama ya umeme

"ilikuwa inang'aa kama ya umeme"

mavazi yake yalikuwameupe kama theluji

"mavazi yake yalikuwa meupe sana kama theluji"

na kuwa kama wafu

Huu ni msemo unaomaanisha kuwa wale maaskari walianguka chini na hawakuweza hata kutikisika. "na walianguka chini na kulala pale kama watu waliokufa"

Matthew 28:5

wale wanawake

"Mariamu Magadalena na yule Mariamu mwingine"

aliyesulibiwa

"yule ambaye watu na maaskari walimsulibisha" au "yula ambaye walimsulibisha"

amefufuka toka wafu

kirai cha "toka wafu" kinamaanisha eneo ambalo roho za wale waliokufa huenda. 'Lakini amefufuka"

mkawaambie wanfunzi wake, 'amefufuka toka wafu. Tazama amewatangulia Galilaya ambako mtamkuta"

waambieni wanafunzi wake kuwa amefufuka wafu na kwamba Yesu amewatangulia kwenda Galilaya ambako mtamwona"

amewatangulia ... mtamwona

kiwakilishi cha "mta" ni cha wingi. kinamaanisha wale wanawake na wanafunzi

nimewaambia

kiwakilishi "wa" ni cha wingi. kinamaanisha wale wanawake

Matthew 28:8

Wale wanawake

"Mariamu Magedalena na Mariamu yule mwingine"

Tazama

neno "Tazama" linatuandaa kusikiliza taarifa zinazofuata. Lugha yako yaweza kuwa namfumo wa kulisema hili.

Salamu

Hii ni salamu ya kawaida

na kushika miguu yake

"walipiga magoti na kugusa miguu yake"

ndugu zangu

Hii inamaanisha wanafunzi wa Yesu.

Matthew 28:11

Sentensi unganishi

Hii inaanza kwa habari ya mwitikio wa viongozi wa dini waliposikia habari ya kufufuka kwa Yesu

Sasa

Hili neno linaonesha mwanzo wa habari kuu. Mathayo anaanza kusimuliasehemu ya habari

wale wanawake

Inamaanisha Mariamu Magadelena na yula Mariamu mwingine

Tazama

Hii inaonesha mwanzo wa tukio lingine katika habari kuu. Inaweza kujumuisha watu tofauti katika matukio yalitangulia. Lugha yako inaweza kuwa na namna ya kulifanya hilo.

kujadili jambo hilo pamoja nao

"walipanga mpango wao wenyewe." Makuhani na wazee waliamua kuwapa zile fedha wale maaskari

Waambieni wengine kuwa, 'wanafunzi wa Yesu walikuja ... wakati tulipokuwa tumelala,'

Wambieni wengine kuwa wanafunzi wa Yesu waikuja ... wakati mlipokuwa mmelala"

Matthew 28:14

Kamataarifa hii itmfikia liwali

"Kama liwali atasikia haya kuwa mlikuwa mmesinzia wakati wanafunzi wa Yesu walipouchukua mwili"

Liwali

"Pilato"

Tutamshawishi na kuwaaondoleeni ninyi mashaka

"msihuzunike. tutongea naye ili asiwaadhibu"

na kufanya kama walivyokuwa wameelekezwa

"walifanya kile ambacho makuhani waliwaambia kufanya"

Habari hii ikaenea sana kwa Wayahudi na imekuwa hivyo hadi leo

"Wayahudi wengi waliisikia habari hii na wanaeendelea kuwaambia wengine hadi leo"

hadi leo

Hii inamaanisha wakati Mathayo alipokuwa akiandika kitabu.

Matthew 28:16

Sentensi unganishi

Hii inaanzisha habari ya Yesu kukutana na wanafunzi wake

walimwabudu, lakini wengine waliona shaka

Maana zake zaweza kuwa 1) wote walimwabudu Yesu ingawa baadhi yao waliona shaka au) Baadhi yao walimwabudu Yesu, lakini wengine hawakumwabudu kwa sababu waliona shaka

lakini baadhi yao waliona shaka

"Wengine wlions shaka kuwa ni kweli yeye ndiye aliyekuwa Yesu na kwamba amefufuka

Matthew 28:18

Nimepewa mamlaka yote

"Baba yangu amaenipa mamlaka yote"

dunuani na mbinguni

"Mbingini" na "duniani"zimetumika pamoja kumaanisha kila kitu na kila mmoja duniani na mbinguni.

mataifa yote

Hapa "mataifa" inamaanisha watu. "kwa watu wote kwa kila taifa"

kwa jina

Hapa "jina" linamaanisha mamlaka. 'kwa mamlaka"

Baba ... Mwana

hIvi ni vyeo maalumu vinavyoonesha uhusiano wa Yesu na Mungu.

Matthew 28:20

"Na azama

"Sikilizeni" au "iweni tayari"

mpaka mwisho wa dunia

"mpaka mwisho wa nyakati" au "mpaka mwisho wa ulimwengu"

Utangulizi wa injili ya Marko

Sehemu ya 1: Utangulizi wa Ujumla

Maelezo ya Kitabu cha Marko

  1. Utangulizi (1:1-13)

  2. Huduma ya Yesu huko Galilaya

  3. Kuelekea Yerusalemu, nyakati mara nyingi ambapo Yesu anatabiri kifo chake mwenyewe; wanafunzi wanakosa kuelewa na Yesu anawafundisha jinsi itakuwa vigumu kumfuata (8:27-10:52)

  4. Siku za mwisho za huduma na maandalizi ya migogoro ya mwisho huko Yerusalemu (11:1-13-13:37)

  5. Kifo cha Kristo na kaburi tupu (14:1-16:8)

Je, kitabu cha Marko kinahusu nini?

Injili ya Marko ni moja ya vitabu vinne katika Agano Jipya ambavyo huelezea baadhi ya maisha ya Yesu Kristo. Waandishi wa Injili waliandika juu ya mambo mbalimbali kuonyesha kuwa Yesu alikuwa nani na ni nini alichofanya. Marko aliandika mengi juu ya jinsi Yesu aliteseka na kufa msalabani. Alifanya hivyo ili kuwatia moyo wasomaji wake ambao walikuwa wakiteswa. Marko pia alielezea desturi za Wayahudi na maneno mengine ya Kiaramu. Hii inaweza kuonyesha kwamba Marko alitarajia wengi wa wasomaji wake wa kwanza kuwa kuwa watu wa mataifa.

Je, kichwa cha kitabu hiki kinapaswa kutafsiriwaje?

Watafsiri wanaweza kuchagua kuita kitabu hiki kwa kichwa chake asilia, "Injili ya Marko" au "Injili Kulingana na Marko." Wanaweza pia kuchagua kichwa ambacho kinaweza kuwa wazi, kama vile "Habari Njema Kuhusu Yesu ambayo Marko Aliandika." (Angalia: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-names)

Nani aliandika Kitabu cha Marko?

Kitabo hakitupatia jina la mwandishi. Hata hivyo, tangu wakati wa Kikristo wa kwanza, Wakristo wengi wamefikiri kwamba mwandishi alikuwa Marko. Marko pia alijulikana kama Yohana Marko. Alikuwa rafiki wa karibu wa Petro. Marko huenda hakushuhudia kile Yesu alichosema na kufanya. Lakini wasomi wengi wanadhani kwamba Marko aliandika katika injili yake kile ambacho Petro alimwambia kuhusu Yesu.

Sehemu ya 2: Mawazo muhimu za Kidini na Kitamaduni

Je, ni njia zipi ambazo Yesu alitumia njia gani kwa kufundisha?

Watu walimwona Yesu kama rabi. Rabi ni mwalimu wa sheria ya Mungu. Yesu alifundisha kwa njia sawa na walimu wengine wa kidini huko Israeli. Alikuwa na wanafunzi ambao walimfuata kila mahali alipoenda. Wanafunzi hawa waliitwa wanafunzi. Mara nyingi aliwaambia mifano. Mifano ni hadithi zinazofundisha masomo ya maadili. (Angalia: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lawofmoses na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#disciple na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#parable)

Sehemu ya 3: Masuala muhimu ya Tafsiri

Je, vitabo vinavyoitwa sinoptiki ni vipi vya Injili ni vipi?

Vitabu vya Mathayo, Marko na Luka huitwa Injili za sinoptiki kwa sababu vina vifungu vingi vinavyofanana. Neno "synoptic" linamaanisha "kuona kwa pamoja."

Maandiko husemekana kuwa "sawa" wakati ambapo injili mbili au tatu zinafanana au zinakaribia kufanana. Wakati wa kutafsiri vifungu sambamba, wafasiri wanapaswa kutumia maneno sawa na kuyafananisha iwezekanavyo.

Je, kwa nini Yesu anajiita mwenyewe kama "Mwana wa Binadamu"?

Katika Injili, Yesu anajiita mwenyewe "Mwana wa Binadamu." Ni kumbukumbu ya Danieli 7:13-14. Katika kifungu hiki kuna mtu anayeelezewa kuwa "Mwana wa binadamu." Hiyo ina maana kwamba mtu huyo alifanana na mwanadamu. Mungu alitoa mamlaka kwa mwana wa binadamu kutawala mataifa milele. Na watu wote watamwabudu milele.

Wayahudi wa wakati wa Yesu hawakutumia "Mwana wa Binadamu" kama jina la mtu yeyote. Kwa hiyo, Yesu aliitumia kwa ajili yake mwenyewe ili kuwasaidia kuelewa yeye alikuwa nani kweli. (Angalia: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sonofman)

Kutafsiri jina "Mwana wa Binadamu" kunaweza kuwa vigumu kwa lugha nyingi. Huenda wasomaji hawaelewi tafsiri halisi. Watafsiri pia wanaweza kutumia jina mbadala, kama vile "Yule aliye Mtu." Inaweza pia kusaidia wanapoingiza maelezo ya chini ili kulielezea.

Je, kwa nini Marko mara nyingi hutumia maneno ambayo yanaashiria muda mfupi?

Injili ya Marko inatumia neno "mara moja" mara arobaini na mbili. Marko hufanya hivyo ili kufanya matukio kuwa ya kusisimua na ya wazi. Inamtoa msomaji haraka kutoka tukio moja hadi linalofuata.

Je, ni yapi masuala makuu katika maandishi ya Kitabu cha Marko?

Aya zifuatazo zinapatikana katika matoleo ya kale ya Biblia lakini hazijajumuishwa katika matoleo ya kisasa zaidi. Watafsiri wanashauriwa kutojumuisha aya hizi. Hata hivyo, ikiwa katika eneo la watafsiri, kuna matoleo ya zamani ya Biblia ambayo yanajumuisha moja au zaidi ya mistari hii, watafsiri wanaweza kuijumuisha. Ikiwa imejumuishwa, inapaswa kuwekwa ndani ya kifungo cha mraba ([]) ili kuonyesha kwamba labda asili yao haikuwa Injili ya Marko.

Kifungu kinachofuata hakipatikani katika maandiko ya awali. Biblia nyingi zinajumuisha kifungu hiki, lakini Biblia za kisasa zimekiweka katika mabango ([]) au zinaonyesha kwa namna fulani kwamba kifungu hiki huenda si mfano ya kitabo cha asili cha Marko ya Injili ya Marko. Watafsiri wanashauriwa kufanya jambo sawa na matoleo ya kisasa ya Biblia.

(See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/jit.html#translate-textvariants)

Mark 1

Marko 01 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri huweka kila mstari wa mashairi kwa upande wa kulia zaidi kuliko maandiko yote ili iwe rahisi kusoma. ULB inafanya hii kwa mashairi katika 1:2-3, ambayo ni maneno kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

"Unaweza kunifanya kuwa safi"

Ukoma ulikuwa ugonjwa wa ngozi ambao ulimfanya mtu asiwe msafi na asiweze kumwabudu Mungu vizuri. Yesu anaweza kufanya watu kuwa "safi" au wenye afya kimwili au pia kuwa "safi" au wenye haki na Mungu kiroho . (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#clean)

"Ufalme wa Mungu umekaribia"

Wasomi wanajadiliana ikiwa "Ufalme wa Mungu" ulikuwapo wakati huu au bado unakuja. Tafsiri za Kiingereza mara nyingi hutumia maneno "karibu," lakini hii inaweza kusababisha ugumu kwa watafsiri. Matoleo mengine hutumia "unakuja" na "umekaribia."

| >>

Mark 1:1

Sentensi ya unganishi

Kitabu cha Marko huanza na nabii Isaya kusema ujio wa Yohana mbatizaji aliye mbatiza Yesu.

Maelezo ya jumla

Mwandishi wa Marko, pia aliyeitwa Yohana Marko, ambaye ni mwana wa mmoja wa wanawake aliyeitwa Mariam aliyetajwa katika injili nne. Pia ni mpwa wa Barinaba.

Mwana wa Mungu

Hii ni jina la muhimu sana kwa Yesu.

Mbele ya uso wako

Hii ni lugha inayomaanisha "mbele yako"

Uso wako... njia yako

Hapa neno "yako" urejea kwa Yesu na liko katika umoja. Pindi unapotafasiri, tumia nomino "yako" kwa sababu ni maneno ya mtu mwingine nabii, na hakutumia jina la Yesu.

Yule

Hii urejee kwa mtumwa.

ataandaa njia yako

Kufanya hivi humaanisha kuandaa watu kwa ajili ya ujio wa Bwana. AT:"nitaandaa watu kwa ajili ya ujio wako"

Sauti ya yule aitae toka jangwani.

Hii inaweza kuelezwa kama sentesi. AT: "Sauti ya yule aitae toka jangwani imesikiwa" au " Wanasikia sauti ya mtu anaita toka jangwani"

Andaa njia ya Bwana... yanyoshe mapito yake

Haya maneno humaanisha kitu kile kile.

Ifanye tayari njia ya Bwana

"Iweke njia tayari ya Bwana." Kufanya hivi humaanisha kuwa tayari kusikia ujumbe wa Bwana unapokuja. Watu hufanya hivi kwa kutubu dhambi zao. AT: "Jiandae kusikia ujumbe wa Bwana unapokuja" au " Tubu na uwe tayari kwa ajili ya Bwana anapokuja"

Mark 1:4

Maelezo ya jumla

Katika mistari hii maneno "yeye" mwanaume, "yule" mwanaume, na "ake" mwanaume urejee kwa Yohana.

Yohana alikuja

Hakikisha wasomaji wako wanaelewa kwamba Yohana alikuwa mtumwa aliyekuwa amenenwa na nabii Isaya katika mistari ya awali.

Nchi yote ya Yuda na watu wote Yerusalemu

Maneno "yote" na "wote" hapa ni maneno ya zaidi hutumiwa kusisitiza kwamba kulikuwa na idadi kubwa ya watu. AT: "Watu wengi kutoka Yuda na Yerusalemu"

Walibatizwa na yeye...kukiri dhambi zao

Haya matendo mawili yalitokewa wakati ule ule. Watu walibatizwa kwa sababu walitubu dhambi zao. AT: "Pindi walipotubu dhambi zao, Yohana aliwabatiza katika mto wa Yordani"

Mark 1:7

Alihubiri

Yohana alihubiri

Sina hadhi hata ya kuinama chini na kufungua kamba za viatu vyake

Yohana anajilinganisha mwenyewe kama mtumishi kuonyesha jinsi gani Yesu ni mkuu. AT:"Sina hadhi na hata kufanya jukumu la chini la kumvulisha viatu vyake.

Ukanda wa ndara zake

Wakati Yesu alipokuwa hai, watu walivaa ndara zilizotengenezwa kwa ngozi na kufungwa kwa ukanda wa ngozi.

Kuinama chini

ni kupinda kwa kuelekea chini

lakini atawabatiza ninyi kwa Roho Mtakatifu

Ubatizo wa kiroho umelinganishwa kwa ubatizo wa maji. Ubatizo wa kiroho huwaleta watu katika mahusiano na Roho Mtakatifu kama ilivyo katika ubatizo wa maji unamleta mtu kuwa uhusiano na maji

Mark 1:9

Wewe ni mwanangu mpendwa

Baba, Mwana, na Roho wote wanajidhihirisha pamoja, kwa wakati mmoja.

alibatizwa na Yohana

Hii inaweza kutajwa katika hali tendaji. AT: " Yohana alimbatiza yeye"

Roho anamshukia kama njiwa

Maana zinazoweza kuwa sahihi ni: 1)huu ni mfanano, na Roho alimshukia Yesu kama ndege anavyoshuka toka mbinguni kuelekea ardhi au 2) Roho kiuhalisia alionekana kama njiwa alivyoshuka juu ya Yesu.

sauti ilisikika toka mbinguni

Hii inawakilisha Mungu anazungumza. Wakati mwingine watu hukwepa kurejea moja kwa moja kwa Mungu kwa sababu wana mheshimu yeye. AT: "Mungu alizungumza toka mbinguni."

mwana mpendwa

Ni neno la cheo kwa Yesu. Baba anamwita Yesu "mwana" kwa sababu ya upendo wa milele kwake.

Mark 1:12

Sentensi unganishi

Baada ya ubatizo wa Yesu, anakuwa nyikani kwa siku arobaini na badae kwenda Galilaya kufundisha na kuita wanafunzi wake.

alimlazimisha kwenda nyikani

"alimwongoza Yesu nje kwa shinikizo"

Alikuwako nyikani

"Alikaa nyikani"

siku arobaini

"muda wa siku arobaini"

Alikuwa pamoja na

"alikuwa miongoni mwa"

Mark 1:14

baada ya Yohana kukamatwa

"Baada ya Yohana kuwa ametiwa gerezani" Hii inaweza kutajwa katika kauli tendaji. AT: " baada ya kumshika Yohana."

alitangaza

"Alihubiri"

Wakati umetimia

"Huu sasa ni wakati"

Mark 1:16

Alimwona Simoni na Andrea

"Yesu alimuona Simoni na Andrea"

kutupa nyavu baharini

Maana pana ya sentensi hii inaweza kuwekwa wazi. AT: "kutandaza wavu katika maji kushika samaki"

Njoo, nifuate mimi

"Nifuate mimi" au "njoo nami"

Nitawafanya kuwa wavuvi wa watu

Huu mfano humaanisha Simoni na Andrea watawafundisha watu ujumbe wa kweli wa Mungu, ili wengine wamfuate Yesu. AT: "Nitakufundisha namna ya kuwapata watu"

Mark 1:19

ndani ya mtumbwi

"ndani ya mtumbwi wao"

kutayarisha nyavu

"kushona nyavu"

aliwaita wao

Inaweza kuwa msaada kusema wazi kwanini Yesu alimwita Yakobo na Yohana. AT: "aliwaita wao waje naye"

watumishi waliokodiwa

"watumishi ambao walifanya kazi kwa ajili yao"

walimfuata

"Yakobo na Yohana walikwenda pamoja na Yesu"

Mark 1:21

Sentensi unganishi

Katika mji wa Kaperinaumu siku ya Sabato Yesu anafundisha katika sinagogi. Anaondoa pepo kwa mtu, ambayo inashanganza watu walio maeneo ya karibu ya Galilaya.

alikuja Kaperinaumu

"alifika Kaperinaumu"

kama mtu aliye na mamlaka na wala siyo mwandishi

Kuna maneno yaliyo achwa katika sentensi hii ambayo yanaweza kuongozwa. AT: "kama mtu aliye na mamlaka alifundisha na siyo kama waandishi wafundishavyo"

Mark 1:23

Tuna nini cha kufanya na wewe, Yesu wa Nazareti?

Mapepo wanauliza swali wakimaanisha kuwa hakuna sababu ya Yesu kuwaingilia na wanatamani yeye aondoke. " Yesu wa Nazareti, tuache sisi peke yetu! Hakuna sababu ya wewe kutuingilia sisi."

Je! Umekuja kutuangamiza sisi?

Mapepo wanauliza swali kumsihi Yesu asiwadhuru. "Usi tuharibu sisi!"

alimtupa yeye chini

Hapa neno "yeye" lina rejea kwa mtu aliye pagawa na mapepo.

wakati analia kwa sauti kubwa

Pepo ndiye anayelia, wala siyo mtu.

Mark 1:27

waliulizana wao kwa wao, "Hiki ni nini? Mafundisho yaliyo na mamlaka?

Mwitikio wa watu unaweza kuandikwa na sentensi hizi badala ya maswali. "walisema wao kwa wao, "Hii ina shanganza! Anatoa mafundisho mapya, na huzungumza na mamlaka!"

Pia ana amru

Neno "yeye" ulerejea kwa Yesu.

Mark 1:29

Sentensi unganishi

Baada ya kumponya mtu aliye pagawa na pepo, Yesu alimponya mama mkwe wa Simoni pamoja na watu wengi wengine.

Sasa mama mkwe wa Simoni alikuwa amelala akiumwa na homa

mkwe alikuwa mgonjwa na homa. Neno "sasa" hutambulisha mama mkwe wa Simoni katika hadidhi na kutupa maelezo ya nyuma kuhusiana yeye.

wachache waliondoka

Inaweza kuonyeshwa waziwazi nani aliye mponya. "Yesu alimponya homa yake"

alianza kuwahudumia

Inamaamisha chakula kilitengwa. "Aliwahudumia chakua la vinywaji"

Mark 1:32

Sentensi unganishi

Hapa maneno "yeye" na "yeye" urejea kwa Yesu.

wote waliokuwa wagonjwa au kupagawa na mapepo

Hapa neno "wote" ni maelezo zaidi na linatumiwa kusisitiza idadi kubwa ya watu waliokuja. "wengi waliokuwa wagonjwa au kupagawa na mapepo."

Mji wote walikusanyika pamoja katika mlango

Neno "wote" linaelezea namba ya watu waliokuwa wakimtafuta Yesu. "Watu wengi kutoka mjini walikusanyika nje ya mlango"

Mark 1:35

Sentensi unganishi

Yesu anachukua muda kuomba katikati ya wakati wake wa kuponya watu. Badae anaenda mjini kupitia Galilaya kuhubiri, kuponya na kutoa mapepo.

Maelezo ya jumla

Hapa maneno "yeye" na "yeye" urejea kwa Yesu

Mahali pa faragha

"mahali ambapo anaweza kuwa peke yake"

Simoni na wale walikuwa naye

Hapa "yeye" urejee kwa Simoni. Pia, wale waliokuwa pamoja naye akiwemo Andrea, Yakobo, Yohana, na inawezekana watu wengine.

Kila mmoja anakutafuta wewe

Neno "kila mmoja" linafafanua namna watu wengi waliomtafuta Yesu. "Watu wengi wanakutafuta wewe"

Mark 1:38

Maelezo ya jumla

Hapa maneno "yeye" na "mimi" urejea kwa Yesu.

Twendeni mahali pengine

"Tunapaswa kwenda mahali pengine." Hapa Yesu anatumia neno "sisi" kurejea kwake, akiwemo Simoni, Andrea, Yakobo, na Yohana.

Alienda akipitia Galilaya yote

Neno "kupitia" linaelezea Yesu alikwenda maeneo mengi wakati wa huduma yake. "Alikwenda maeneo mengi ya Galilaya."

Mark 1:40

Mwenye ukoma alikuja kwake; alikuwa akimsihi wakati amepiga magoti na kumwambia

"Mwenye ukoma alikuja kwa Yesu; mwenye ukoma alikuwa akimsihi Yesu akiwa amepiga magoti chini. Mwenye ukoma alisema kwa Yesu"

Kama unataka, unaweza kunifanya safi

Kikundi cha maneno "kunifanya safi" kinaeleweka kutoka kwenye kikundi kingine cha maneno. "Kama unataka kunifanya safi, basi unaweza kunifanya safi."

uko tayari

"nataka" au "hamu"

unaweza kunifanya niwe safi

Nyakati za Biblia, mtu aliye kuwa na ugonjwa wa ngozi alihesabika siyo msafi mpaka pale ngozi ilipo ponywa na kubaki bila kuwa na maambukizi. "unaweza kuniponya"

Alisukumwa na huruma, Yesu

Hapa neno " kusukumwa" ni lugha inayo maanisha kuwa na hisia juu ya hitaji la mtu mwingine. "Kuwa na huruma kwa ajili yake, Yesu "au" Yesu alipatwa na huruma kwa ajili ya mtu.

Nina utayari

Inaweza kuwa msada kutaja kitu gani Yesu ana utayari kufanya"Ninatamani kukufanya uwe safi"

Mark 1:43

Maelezo ya jumla

Neno "yeye" ni limetumiwa kurejea kwa yule mkoma aliyeponywa na Yesu.

Uwe na uhakika kutosema chochote kwa yoyote.

"Uwe na uhakika kutosema chochote kwa yoyote"

jionyeshe mwenyewe kwa kuhani

Yesu alimwambia mtu kujionyesha mwenyewe kwa kuhani ili kuhani aweze kumuona ngozi yake kama kwamba ukoma wake umekwisha. Ilihitajika katika sheria ya Musa mtu kujionyesha kwa kuhani kama amekuwa safi.

jionyeshe mwenyewe

Neno "mwenyewe" linawakilisha ngozi ya mwenye ukoma. "jionyeshe ngozi yako"

ushuhuda kwao

Ni vizuri kutumia nomino "wao", kama inawezekana, katika lugha yako. Maana zinazowezekana ni 1) "ushuhuda kwa makuhani" 2) "ushuhuda kwa watu"

Mark 1:45

Lakini alienda

Neno "yeye" urejea kwa mtu aliyeponywa na Yesu.

mwambie kila mmoja...sambaza neno

vivumishi vya maneno haya mawili yana maana inayofanana na yanamwelezea yule mtu aliyewaambia watu wengi.

kila mmoja

Neno "kila mmoja" linafafanua, "Watu wengi aliokutana nao."

Yesu hakuweza tena kuingia mjini kwa uhuru

Hii ina maanisha kwamba makundi makubwa yalimzuia Yesu kuingia mjini kwa sababu makundi yalifanya ugumu kwake kutembea katika mji. "makundi yalimzuia Yesu kutembea kwa uhuru mjini."

mahali pa faraga

"mahali pa utulivu" au "mahali ambapo hakuna mtu aliye ishi"

kutoka kila mahali

Neno "kila mahali" linafafanua kuwa, "kutoka maeneo yote ya mkoa"

Mark 2

Marko 02 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

"Wenye dhambi"

Watu wa wakati wa Yesu walipozungumza juu ya "wenye dhambi," walikuwa wakiongea juu ya watu ambao hawakuitii sheria ya Musa na badala yake wakatenda dhambi kama kuiba au dhambi za ngono. Wakati Yesu alisema kwamba alikuja kuwaita "wenye dhambi," alimaanisha kwamba watu pekee wanaoamini kuwa wao ni wenye dhambi wanaweza kuwa wafuasi wake. Hii ni kweli hata kama wao sio wale ambao watu wengi wanafikiria kuwa "wenye dhambi." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

Kufunga na Karamu

Watu wangeweza kufunga, au kutokula chakula kwa muda mrefu, walipokuwa na huzuni au wakimwonyesha Mungu kwamba walijutia dhambi zao. Wakati walipokuwa na furaha, kama wakati wa harusi, wangekuwa na karamu, au mlo ambapo wangeweza kula chakula kikubwa. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#fast)

Takwimu muhimu za hotuba katika sura hii

Maswali ya uhuishaji

Viongozi wa Kiyahudi walitumia maswali ya uhuishaji ili kuonyesha kwamba walikuwa wamekasirika kwa sababu ya kile Yesu alichosema na kufanya na kwamba hawakuamini kwamba alikuwa Mwana wa Mungu (Marko 2:7). Yesu aliyatumia kuonyesha viongozi wa Kiyahudi kwamba walikuwa wenye kiburi (Marko 2:25-26). (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-rquestion)

<< | >>

Mark 2:1

Sentensi unganishi

Baada ya kuhubiri na kuponya watu kote Galilaya, Yesu anarudi Kaperinaumu anako mponywa na kumsamehe dhambi mtu aliye pooza

Ilisikika kwamba alikuwa nyumbani

Hii inaweza kutajwa katika kauli tendaji. watu wa pale walisikia kwamba alikuwa katika nyumba ile ile.

wengi walikusanyika hapo

Hii inaweza kutajwa kama kauli tendaji. "kwa hiyo watu wengi walikusanyika" au "watu wengi walikuja nyumbani"

haikuwepo nafasi ya ziada

Hii inarejea hapakuwa na nafasi ndani ya nyumba. "haikuwepo nafasi tena kwa ajili yao mule ndani"

Mark 2:3

watu wanne walimbeba yeye

"wanne wao walimbeba yeye." Inawezekana kulikuwa na watu zaidi ya wanne ndani ya kundi waliomleta mtu kwa Yesu.

walimletea mtu aliyepooza

walimletea mtu asiyeweza kutembea wala kutumia mikono yake.

Walishindwa kumkaribia yeye

"walishindwa kukaribia pale Yesu alipokuwa Yesu"

waliondoa paa juu alipokuwa...kutoboa tundu ndani yake

Nyumba alizoishi Yesu zilikuwa na paa za wima zilizo tengenezwa kwa udongo na kufunikwa kwa vigaye. Hatua ya kutengeneza tundu juu ya paa inaweza kuelezwa zaidi kwa uwazi au kufanywa zaidi kwa ujumla ili kwamba iweze kueleweka katika lugha yako. "waliondoa vigaye sehemu ya paa juu alikokuwa Yesu. Na walipotoboa katika paa ya udongo "au" walipotengeneza tundu juu ya paa alipokuwa Yesu, na kisha walimshusha"

Mark 2:5

alipoiona imani yao.

"Akijua kwamba watu hao wana imani." Hii inaweza kumaanisha 1) kwamba ni wale watu waliokuwa wamembeba aliyepooza ndio waliokuwa na imani au 2) kwamba aliyepooza na watu wamembeba wote walikuwa na imani.

Mwana

Neno "mtoto" hapa linaonesha kwamba Yesu alimjali huyo mtu kama baba anavyomjali mwana.

dhambi zako zimesamehewa

Maana zinayowezekana 1) "Mungu amekwisha kukusamehe dhambi zako" (Taz 2:7) au 2) "Nimekusamehe dhambi zako."

walijihoji mioyoni mwao

Hapa "mioyo yao" ni mbadala wa mawazo ya watu. "walikuwa wanafikiri wao wenyewe"

Anawezaje mtu huyu kusema hivi?

Hili swali liliulizwa kuonyesha kwamba waandishi walitilia shaka uwezo wa Yesu kusamehe dhambi. "Mtu huyu hapaswi hivi!"

Nani anayeweza kusamehe dhambi isipokuwa Mungu peke yake?

Swali hili liliulizwa kuonyesha kwamba waandishi walitia shaka kwamba Yesu ni Mungu. "Mungu peke yake ndiye anaweza kusamehe dhambi!"

Mark 2:8

katika roho yake

"ndani ya utu wa ndani" au"ndani yake"

walikuwa wakifiri miongoni mwao wenyewe

Waandishi walikuwa wakifiri kila mmoja nafsini mwake; walikuwa hawaongeleshani kila mmoja na mwenzake.

Kwa nini mnafikiri hivi mioyoni mwenu?

Yesu aliuliza swali hili kuwakemea waandishi kwa kutilia mashaka mamlaka yake. NI kama alitaka kusema kuwa, "Hampaswi kuonea shaka mamlaka yangu!"

hii iko ndani ya mioyo yenu

Neno "mioyo" linatumika mara kwa mara kurejea kwenye mawazo, hisia, matamanio, au mapenzi ya mtu

Lipi ni jepesi kusema kwa mtu aliyepooza... chukua kitanda, na utembee?

Yesu aliuliza swali hili kwa sababu waandishi waliamini kwamba mtu huo alikuwa amepooza kwa sababu ya dhambi zake na ikiwa dhambi za mtu huyo zingesahewa, angeweza kutembea. Kama Yesu alimponya mtu aliyepooza, waandishi walipaswa kukiri kwamba Yesu anaweza kusamehe dhambi. Sawa na kusema "Ni rahisi kumwambia mtu aliyepooza dhambi zako zimesamehewa!" [Hili ni swali lisihitaji jibu]

Mark 2:10

Lakini ili kwamba umjue

"Lakini ili kwamba umjue." Neno "wewe" urejea kwa waandishi na kundi.

kwamba Mwana wa Adamu ana mamlaka

Yesu ujirejea yeye mwenyewe kama "Mwana wa Adamu." "Kwamba mimi ni Mwana wa Adamu na nina mamlaka."

mbele ya kila mmoja

"wakati watu walipokuwa wakitazama"

Mark 2:13

Sentensi unganishi

Yesu anafundisha kundi kando ya bahari ya Galilaya, na anamwita Lawi kumfuata yeye.

ziwa

Hili ni bahari la Galilaya, ambayo linajulikana kama ziwa la Gennesareti.

mkutano ulikuja kwake

watu walikwenda pale alipokuwa

Lawi mwana wa Alfayo

Alfayo ni baba wa Lawi

Mark 2:15

Sentensi unganishi

Ni badae sasa kwa siku hiyo, na Yesu anakuwa katika nyumba ya Lawi kwa ajili ya chakula.

Nyumba ya Lawi

"nyumba ya Lawi"

watu wenye dhambi

Mafarisayo walitumia kikundi cha maneno "watu wenye dhambi" kurejea kwa watu walioshindwa kutunza sheria kama walivyo fikiri Mafarisayo wangefanya.

kwa kuwa kulikuwa na wengi na walimfuata

Maana zinazowezekana ni 1) "kulikuwa na watoza kodi wengi na watu waovu waliomfuata Yesu

kwa nini anakula na wakusanya kodi na watu wenye dhambi?

Waandishi na Mafarisayo waliuliza swali hili konesha kwamba walikataa ukarimu wa Yesu. "Hakupaswa kula na kunywa na wenye dhambi na watu wanaokusanya kodi."

Mark 2:17

Sentensi unganishi

Yesu aliitikia kwa kile walichokuwa wamesema waandishi kwa wanafunzi wake kuhusu kula na watoza kodi na watu wenye dhambi.

aliwaambia

aliwaambia waandishi

Watu walio na nguvu katika mwili hawamhitaji tabibu; ni wagonjwa pekee ndio wanamhitaji

Yesu aliwalinganisha wale wanajijua kuwa ni wenye dhambi na wale wale wanaojijua kuwa ni wagonjwa. "Watu wanaofikiri kuwa wao ni wenye haki hawahitaji msaada; ni wale tu wanaojijua kuwa ni wagonjwa ndio wanaohitaji msaada!

nguvu katika mwili

"afya"

Sikuja kuwaita watu wenye haki, lakini watu wenye dhambi

Yesu alitegemea kuwa wasikilizaji wake wangeelewa kwamba alikuja kwa wale wanaohitaji msaada. "Nilikuja kwa watu wanaojielewa kuwa ni wenye dhambi, siyo kwa watu wanaoamini kuwa wao ni wenye haki."

lakini watu wenye dhambi

Inaweza kuwa msaada kutaja kwamba hii inarejea kwa watu ambao Yesu aliwaita. "lakini nilikuja kuwaita watu wenye dhambi"

Mark 2:18

Sentensi unganishi

Yesu anasema mifano kuonyesha kwa nini wanafunzi wake hawakuweza kufunga pindi alipokuwa nao.

Mafarisayo walifunga...wanafunzi wa Mafarisayo

Haya maneno yanarejea kwa kundi lile lile la watu, lakini la pili liko bayana zaidi. Yote urejea kwa wanafunzi wa Mafarisayo, lakini hayalengi kwa viongozi wa Mafarisayo. "wanafunzi wa Mafarisayo walikuwa wakifunga... wanafunzi wa Mafarisayo"

baadhi ya watu

"baadhi ya watu." Ni vizuri kutofasiri kikundi cha maneno bila bayana hawa walikuwa watu akina nani. Kama katika lugha yako unapaswa kuwa bayana, maana zinazowezekana ni 1)hawa watu hawakuwa miongoni mwa wanafunzi wa Yohana au wanafunzi wa Mafarisayo au 2) hawa watu walikuwa miongoni mwa wanafunzi wa Yohana

Je waliohudhuria harusini wanaweza kufunga wawkati bwana harusi akiwa yuko bado pamoja nao?

Yesu aliuliza swali hili kulinganisha kati yake mwenyewe na wanafunzi wake na bwana harusi na marafiki wake.'' wanafunzi wangu husherekea kwa kuwa niko pamoja nao!''

Mark 2:20

bwana harusi atakapoondolewa

Yesu anajilinganisha mwenyewe na bwana harusi anapoongelea kuhusu kifo chake, ufufuo na kupaa kwake. Kama lugha yako inakulazimu kuchanganua mtendaji, fanya kwa ujumla kama iwezekanavyo. Kauli ya kutenda inachukua nafasi kama lugha yako haiwezi kutumia kauli ya kutendewa. "Watamwondoa bwana harusi" au bwana harusi ataondoka."

mbali nayo... wao watafunga

Neno "kwao" na "wao" urejea kwa washiriki wa harusi.

Hakuna mtu ashonaye kipande kipya cha nguo kwenye vazi kuukuu

Kushona kipande kipya cha nguo kwenye vazi kuukuu kitasababisha tundu kwenye vazi kuukuu kuwa baya zaidi kama kipande cha nguo mpya hakitabadilika. Vyote viwili, nguo mpya na vazi kuukuu vitapotea.

Hakuna mtu

"Hakuna yoyote." Kikundi cha maneno urejea kwa watu wote, wala siyo watu.

Mark 2:22

Hakuna mtu atiaye divai mpya katika viriba vikuukuu

Yesu analinganisha mafundisho yake na wanafunzi wake na divai mpya na viriba vipya. Mfano huu hujibu swali "Kwa nini wanafunzi wa Yohana na wa Mafarisayo wanafunga, lakini wanafunzi wako hawafungi? Hapa "Hakuna mtu akabidhiye mafundisho mapya kwa wale waliozoea mafundisho ya zamani."

Divai mpya

"juice ya zabibu." Hii ina maana ya mvinyo ambayo haijaumuka bado. Kama zabibu hazijulikani katika eneo lako, tumia neno la jumla kwa matunda.

virriba vikuukuu

Hii inamaanisha viriba ambavyo vimetumika mara nyingi

viriba

Hii ilikuwa mifuko iliyotengenezwa kwa kutumia ngozi za wanyama. Pia inaweza kuitwa "mifuko ya divai" au "mifuko ya ngozi" (UDB)

divai itaweza kuvipasua viriba

Wakati divai mpya inapoumuka na kupanuka, inaweza kupasua na kutoka nje kwa sababu havitaweza tena kunyooka kwa nje.

kupotea

kuharibika

viriba vipya

"viriba vipya" au "mifuko mipya ya divai." Hii inarejea kwa viriba vipya ambavyo havijawahi kutumika.

Mark 2:23

Sentensi unganishi

Yesu anawapa Mafarisayo mfano kutoka katika maandiko kuonyesha kwanini wanafunzi hawakuwa sahihi kuchukua masuke ya ngano siku ya Sabato.

kuchukua masuke ya ngano...kufanya kitu ambacho siyo sawa kisheria katika siku ya Sabato

Kuchukua ngano katika mashamba ya wengine na kula haikuhesabiwa kuwa wizi. Swali lilikuwa kama ilikuwa sawa kufanya jambo kama hilo siku ya Sabato

kuchukua masuke ya ngano

Wanafunzi walichukua masuke ya ngano kuyala. Hii inaweza kuelezwa kwa maneno kuonyesha maana kamili. "chukua na kula masuke ya ngano"

masuke ya ngano

Hii ni sehemu nyeti ya zao la ngano, ambayo ni aina ya nyasi pana. Hushikiria ngano iliyokomaa au mbegu za mmea

Tazama, kwanini wanafanya kitu ambacho ni kinyume na sheria katika siku ya Sabato?

Mafarisayo wanamuuliza Yesu swali kumlaani. Hii inaweza kutofasiriwa kama sentensi. "Tazama! Wanavunja sheria ya kiyahudi kuhusu Sabato"

Tazama

"Uwe makini kusikiliza kile ninachotaka kukuambia"

Mark 2:25

Aliwambia

"Yesu aliwambia Mafarisayo"

Hamjasoma kile alichofanya Daudi pamoja naye? Jinsi alivyokwenda

Yesu alijua kwamba Waandishi na Mafarisayo walikuwa wamesoma simulizi. Aliwashutumu kwa kukuielewa kwa makusudi. Tafsiri mbadala: "Kumbukeni kile Daudi alichofanya...pamoja naye na jinsi alivyokwenda" au "Kama mnakumbuka kile Daudi...naye, mngejua kwamba alikwenda"

Hamkusoma kile alichofanya Daudi alipokuwa katika uhitaji na njaa-- yeye pamoja na watu waliokuwa pamoja naye

Hii inaweza kusema kama amri. "Kumbuka ulichosoma kuhusu alichofanya Daudi wakati ambapo alikuwa na watu wakiwa na uhitaji na njaa"

soma nini Daudi

Yesu anarejea kwa kusoma kuhusu Daudi katika Agano kale. Hii inaweza kutofasiriwa kuonyesha taarifa thabiti.

Jinsi alivyokwenda katika nyumba ya Mungu...kwa wale walikuwa naye?

Hii inaweza kuelezwa kama sentensi iliyotengenishwa na mstari wa 25. "Alienda aliingia katika ya Mungu...kwa wale walikuwa naye" (UDB)

namna gani alienda

Neno "a" urejea kwa Daudi

mkate uliowekwa mbele

Hii urejea kwa mikate kumi na miwili ambayo ilikuwa imewekwa kwenye meza ya dhahabu ndani ya hema au jengo la hekalu kama dhabihu kwa Mungu nyakati za kipindi cha Agano la Kale.

Mark 2:27

Sabato ilifanywa kwa ajili ya mwanadamu

"Mungu aliweka Sabato kwa ajili ya mwanadamu"

mwanadamu

"mtu" au "watu" au "mahitaji ya watu" Hii urejea kwa wanaume na wanawake.

siyo mwanadamu kwa ajili ya Sabato

'Mungu hakumuumba mtu kwa ajili ya uzuri wa Sabato"

Mark 3

Marko 03 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Sabato

Ilikuwa kinyume cha sheria ya Musa kufanya kazi siku ya sabato. Mafarisayo waliamini kumponya mtu mgonjwa siku ya Sabato ilikuwa "kazi," hivyo wakasema kwamba Yesu alifanya makosa wakati alimponya mtu siku ya Sabato. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lawofmoses)

"Kukufuru dhidi ya Roho"

Hakuna mtu anayejua kwa hakika hatua ambazo watu hufanya au maneno gani wanayosema wanapotenda dhambi hii. Hata hivyo, labda wao humtusi Roho Mtakatifu na kazi yake. Sehemu ya kazi ya Roho Mtakatifu ni kuwafanya watu kuelewa kuwa wao ni wenye dhambi na wanahitaji kusamehewa na Mungu. Kwa hiyo, yeyote asiyejaribu kuacha dhambi huenda anakufuru Roho. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#blasphemy and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#holyspirit)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Wanafunzi kumi na wawili

Yafuatayo ni orodha ya wanafunzi kumi na wawili:

Katika Mathayo:

Simoni (Petro), Andrea, Yakobo mwana wa Zebedayo, Yohana mwana wa Zebedayo, Filipo, Bartholomeo, Tomasi, Mathayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Tadayo, Simoni wa Zeloti na Yuda Isikariote.

Katika Marko:

Simoni (Petro), Andrea, Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana mwana wa Zebedayo (ambao aliwaita Boanerge, yaani, wana wa ngurumo), Filipo, Bartholomeo, Mathayo, Tomasi, Yakobo mwana wa Alifayo, Tadayo Simoni wa Zeloti na Yuda Isikariote.

Katika Luka:

Simoni (Petro), Andrea, Yakobo, Yohana, Filipo, Bartholomeo, Mathayo, Tomasi, Yakobo mwana wa Alifayo, Simoni (aitwaye Zeloti), Yuda mwana wa Yakobo, na Yuda Isikariote.

Thadayo labda ni Yuda, mwana wa Yakobo.

Ndugu na Dada

Watu wengi huwaita wale ambao wana wazazi sawa "ndugu" na "dada" na kuwafikiria kama watu muhimu zaidi katika maisha yao. Watu wengi pia huita wale walio na babu na nyanya sawa "ndugu" na "dada." Katika sura hii Yesu anasema kwamba watu muhimu zaidi kwake ni wale wanaomtii Mungu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#brother)

<< | >>

Mark 3:1

Sentensi unganishi

Yesu amponya mtu siku ya Sabato katika Sinagogi na kuonyesha jinsi anavyojisikia walivyofanya Mafarisayo kuhusiana na sheria za Sabato. Mafarisayo na Maherode wanapanga kumua Yesu.

Baadhi ya watu

"Baadhi ya Mafarisayo." Badae, katika 3:5, hawa watu wanaonyeshwa kama Mafarisayo.

mtu aliye na mkono uliopooza

"mtu aliye na mkono uliopooza"

Baadhi ya watu walimtazama kuona kama atamponya

"Mafarisayo walimtazama Yesu kwa karibu sana kuona kama atamponya na mkono uliopooza"

mshtaki

Mafarisayo walitaka kumshtaki Yesu kwa kuvunja sheria kwa kufanya kazi siku ya Sabato, je amponye mtu. "kumshtaki yeye kwa kufanya kosa" au " kumshtaki yeye kwa kuvunja sheria"

Mark 3:3

katika ya umati

"katika ya umati huu"

Je ni halali kutenda tendo jema siku ya Sabato... au kutenda yasiyo haki?

Yesu alisema changamoto hii. Alitaka wao wakiri kuwa ni halali kumponya mtu siku ya Sabato.

kutenda tenda jema siku ya Sabato au kutenda isivyo haki... kuokoa maisha au kuua.

Haya makundi ya maneno yanafanana katika maana, tofauti ya pili imeenda ndani zaidi.

kuokoa maisha, au kuua

Inaweza kuwa ni msaada kutubu "ni halali," kama lilivyo swali analouliza Yesu tena kwa njia nyingine. "ni halali kuokoa maisha au kuua"

maisha

Hii urejea kwa maisha ya kimwili kama neno mbadala kwa mtu. "mmoja wapo anakufa" au maisha ya mmoja wapo"

Lakini walikuwa kimya

"Lakini walikataa kumjibu"

Mark 3:5

Aliangalia

"Yesu aliangalia"

alihuzunika

"alikuwa na huzuni kubwa"

ugumu wa mioyo yao

Huu mfano unaelezea jinsi Mafarisayo hawakuwa tayari kuwa na huruma kwa huyo mtu aliye kuwa na mkono uliopooza. "hawakuwa tayari kuwa na huruma kwa mtu huyo"

Nyosho mkono wako

"Nyosha mkono wako"

mkono wake uliponywa

Hii inaweza kutajwa na kauli tendaji. "Yesu alimponya mkono wake" au Yesu aliufanywa mkono wake kama ulivyo kuwa awali"

wakafanya njama

walianza kufanya mpango

Maherode

Hili ni jina la kisiasa lilompa nguvu Herode wa Antipasi

kwa namna gani watamuua

"kwa namna gani watamuua Yesu"

Mark 3:7

Sentensi unganishi

Yesu aliendelea kuponya watu kama alivyofuatwa na umati mkubwa pindi alipotaka kuwa mbali nao.

bahari

Hii urejea bahari ya Galilaya

Idumaya

Huu ni mkoa, hapo awali ulijulikana kama Edomu, ambao ulikuwa mpaka nusu ya kusini mwa mkoa wa Uyahudi.

mambo aliyokuwa anafanya

Hii inarejea kwa miujiza ya Yesu aliyokuwa akifanya. "miujiza mikubwa aliyokuwa akifanya"

alikuja kwake

"alikuja alipokuwa Yesu"

Mark 3:9

Na aliwaambia wanafunzi wake kuwa na mtubwi mdogo... ili kwamba wasije wakamsonga.

Kama ilivyokuwa umati mkubwa ulikuwa unamsonga Yesu, alikuwa katika hatari ya kusongwa. Katika mstari wa 9-10 yameunganishwa na kusemwa taarifa dhabiti kwa usahihi.

aliwauliza wanafunzi wake

"Yesu aliwambia wanafunzi wake"

Kwa kuwa aliponya wengi, ili kwamba

Neno "wengi" umaanisha idadi kubwa ya watu waliokwisha ponywa na Yesu. "Kwa sababu Yesu alikuwa ameponya tayari watu wengi, kila mmoja"

yeyote aliyekuwa na mateso alikuwa na shauku ya kumsogelea ili kwamba amguse.

"wagonjwa wote walimsonga wakiwa na shauku ya kumgusa"

Mark 3:11

muone yeye

"muone Yesu"

walianguka...wakalia na kusema

Hapa "wao" urejea kwa roho chafu. Ni zile zinazosababisha watu wanao wamiliki kufanya mambo. Hii inaweza kufanywa dhabiti. "ziliwasababisha watu wanao wamiliki kuanguka chini mbele yake na kulia.

walianguka mbele yake

Roho chafu hazikuanguka mbele yake Yesu kwa sababu zilimpenda au zilitaka kumwabudu yeye. Zilianguka chini mbele yake kwa sababu zilimuogopa.

Wewe ni Mwana wa Mungu

Yesu ana nguvu juu ya roho chafu kwa sababu ni yeye ni "Mwana wa Mungu"

Mwana wa Mungu

Hili ni jina la muhimu sana kwa Yesu

Aliwaamuru kwa msisitizo

"Yesu aliwaamuru kwa msisitizo roho hizo chafu"

si kumfanya yeye ajulikane

"si kumfunua yeye ni nani"

Mark 3:13

Sentensi unganishi

Yesu awaita rasmi wanafunzi wake kabla hajaenda nyumbani, pale aliposhitakiwa kuwa wazimu na aliyetawaliwa na Beelzebuli.

ili kwamba wawe pamoja naye na aweze kuwatuma kuhubiri

"ili kwamba wawe pamoja naye na aweze kuwatuma kuhubiri"

Simoni, aliyempa jina la Petro

Mwandishi anaanza kuwataja orodha ya majina ya mitume kumi na mbili. Simoni ni mtu wa kwanza aliye kutajwa.

Mark 3:17

kwa wale aliowapa

Kikundi cha maneno "kwa wale" urejea kwa wote Yakobo mwana wa Zebedayo na ndugu yake Yohana.

jina la Bonagesi, hao ni, wana wa ngurumo

"Jina Bonagesi, ambalo lina maanisha wana wa ngurumo" Maana ya jina "Bonagesi" inaweza kuwa dhabiti zaidi. "jina jipya 'wanaume wanaofananishwa kama ngurumo"

Thadayo

Hili ni jina la mwanaume

ambaye atamsaliti

"ambaye atamsaliti Yesu" Neno "ambaye" urejea kwa Yuda Iskariote.

Mark 3:20

Kisha alienda nyumbani

"Kisha Yesu alienda nyumbani kule alikokuwa anaishi"

kula mkate

Neno "mkate" usimama badala ya chakula. "kule wote" au " kula chochote"

walienda kumkamata

Familia yake walienda nyumbani, ili kwamba wamkamate na kumlazimisha aende nao.

kwani walisema

Maana za neno "wao" ni 1) ndugu zake au 2) baadhi ya watu katika umati

amerukwa na akili zake

"Familia ya Yesu inatumia lugha hii kueleza kwa namna gani wanafikiri anavyofanya. "uazimu" au kichaa"

Kwa mtawala wa mapepo anatoa mapepo

"Kwa nguvu za Beelzebuli ambaye ni mtawala wa mapepo, Yesu anatoa mapepo

Mark 3:23

Sentensi unganishi

Yesu aeleza kwa mifano kwanini hatawaliwi na Shetani na wale wanaofanya mapenzi ya Mungu wako vile vile kama kuwa kaka yake, na dada, na mama.

Yesu aliwaita kwake

"Yesu aliwaita watu waje kwake"

Inawezekanaje Shetani kumtoa Shetani?

Yesu aliuliza swali hili katika kuwajibu waandishi kusema kwamba anatoa mapepo kwa Beelzebuli. " "Shetani hawezi kujitoa yeye mwenyewe!" au " Shetani hawezi kwenda kinyumbe na roho zake chafu!"

Kama ufalme umegawanyika yenyewe

Neno "ufalme" ni neno mbadala kwa watu wanaoishi katika ufalme. "kama watu wanaoishi katika ufalme wamegawanyika wao wenyewe"

haiwezi kusimama

Kikundi hiki cha maneno ni mfano wa maana kwamba watu hawataunganishwa na wataanguka. "hawatavumilia" au "wataanguka"

nyumba

Haya ya maneno mbadala kwa watu wanaoishi ndani ya nyumba. "familia" au "kaya"

Mark 3:26

Kama Shetani atainuka kinyume chake mwenyewe na kugawanyika

Neno "mwenyewe" ni nomino tendaji ambayo inarejea tena kwa Shetani, na mfano mbadala wa roho chafu zake. "Kama Shetani na roho zake chafu waligombana" au "kama Shetani na roho zake chafu wameinukiana dhidi ya mwenzake na wamegawanyika"

hawezi kusimama

Huu ni mfano unamaanisha ataanguka na hawezi kuvumilia. "atakoma kuwa pamoja" au "hawezi kuvumilia na amefika mwisho" au "ataanguka na amefika mwisho.

mnyang'anyi

kuiba vitu vya dhamani vya mtu

Mark 3:28

Kweli nawambieni

Hii huonyesha kwamba sentensi inayofuata ni ya kweli na muhimu

wana wa watu

"wale waiokwisha zaliwa." Sura hii imetumiwa kusisitiza ubinadamu wa watu. "watu"

tamka

"zungumza"

walikuwa wakisema

"watu walikuwa wakisema"

ana roho chafu

Hii ni lugha inayo maanisha kumilikiwa na roho chafu. "anamilikiwa na roho chafu"

Mark 3:31

ndugu

Hii inarejea kwa ndugu zake Yesu

Wakamtuma mtu, kumwita

"Wakamtuma mtu ndani kumwambia kwamba walikuwa nje na kwamba yeye anapaswa kuja kwao"

wanakutafuta wewe

"wanakuulizia wewe"

Mark 3:33

huyu ndugu yangu, dada, na mama

"hawa ni ndugu, dada yangu, na mama yangu"

Mark 4

Marko 04 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Marko 4:3-10 huunda mfano mmoja. Mfano huo umeelezwa katika 4:14-23.

Baadhi ya tafsiri huweka kila mstari wa mashairi upande wa kulia zaidi kuliko maandiko yote ili iwe rahisi kusoma. ULB inafanya hivyo kwa mashairi katika 4:12, ambayo ni maneno kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

Mifano

Mifano ni hadithi fupi ambayo Yesu aliwaambia ili watu waweze kuelewa kwa urahisi somo alilojaribu kuwafundisha. Pia aliwaambia hadithi ili wale ambao hawakutaka kumwamini wakose kuelewa kweli.

<< | >>

Mark 4:1

Sentensi unganishi

Yesu alipokuwa anafundisha akiwa kwenye mtumbwi kandokanod ya bahari, aliwambia mfano wa udongo

bahari

Hii ni bahari la Galilaya

na kukaa chini

"na akaketi ndani mwa mtumbwi"

Mark 4:3

Sikilizeni

"Zingatia"

Alipokuwa akipanda

"Alipokuwa akipanda mbengu juu ya udongo." Kwa tamaduni zingine watu walipanda mbingu kwa utofauti. Katika mfano huu mbengu zilipandwa kwa kutupwa juu ya ardhi iliyokuwa imeandaliwa kwa kukuza.

ziliota

"zilianza kuota kwa haraka"

udongo

Hii inarejea kupoteza uchafu juu ya ardhi ambapo utapanda mbengu.

Mark 4:6

zilinyauka

Hii urejea kwa mimea midogo. Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "inanyausha mimea midogo"

sababu hazikuwa na mzizi

"sababu mimea midogo haikuwa na mizizi, zilinyauka"

na ikazisonga

Neno ika -"zi"-songa urejea kwa mimea midogo

Mark 4:8

zingine zilizaa mara thelathini zaidi

Kiasi cha nafaka kilichotokana na kila mmea inalinganishwa na mbengu moja iliyoota. "Mimea baadhi ilizaa mara thelathini zaidi kama mbegu ilivyopandwa na mtu"

thelathini...sitini...na mia

"30...60...100." Hizi zinaweza kuandikwa kama hesabu

na baadhi sitini, na baadhi mia

Yesu anaendelea kueleza kiasi cha nafaka iliyopatikana. Udondoshaji wa maneno umetumika hapa kufupisha kikundi cha maneno lakini yanaweza kuandikwa. "na baadhi zilizaa sitini zaidi ya nafaka na baadhi zilizaa mia zaid ya nafaka"

Yeyote aliye na masikio kusikia

Hii ni njia ya kurejea kwa yeyote asikilizae. "Yeyote anayenisikiliza mimi"

acha asikilize

Hapa neno "kusikiliza" humaaanisha kuwa makini. "unapaswa kuwa makini kwa kila ninachosema"

Mark 4:10

Yesu alipokuwa peke yake

Hii haimaanishi kwamba Yesu alikuwa kabisa peke yake, hapa, umati wa watu ulikuwa umeenda na Yesu alikuwa na wanafunzi kuma na wawili na wafuasi wengine baadhi.

Kwenu mmepewa

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "Mungu amekupa wewe" au "Nimekwisha kukupa wewe"

kwa walio nje

"lakini kwa wale hawako miongoni mwenu" Hii urejea kwa wote wale hawakuwa miongoni mwa wanafunzi kumi na wawili au wafuasi wengine wa Yesu.

kila kitu kiko katika mifano

Inaweza kusemwa kwamba Yesu anatoa mifano kwa watu. " Nimezungumza vyote katika mifano"

wanapotazama... wanaposikia

Inakisiwa kwamba Yesu anazungumza kuhusu watu akitazama kwa kile anacho waonyesha na kusikia kile anacho wambia. "wanapotaza kile nafanya... wanaposikia kile nachosema "

wanatazama, lakini hawaoni

Yesu anazungumzia watu wanaoelewa wanachokiona kwa uhalisia. "wanatazama na hawaelewi"

geuka

Hii inamaanisha kugeuka mbali na dhambi

Mark 4:13

Sentensi unganishi

Yesu anaelezea mfano wa udongo kwa wafuasi wake na kisha anawambia kuhusiana na taa kuonyesha vitu vilivyo jificha vitajulikana.

Na akasema kwao

"Na Yesu akasema na wanafunzi wake"

Je hamuelewi mfano huu? Mtawezaje kuelewa mifano mingine ?

Yesu alitumia maswali haya kuonyesha jinsi alivyokuwa na huzuni kwamba wanafunzi wake hawakuweza kuelewa mfano wake. "kama hautaweza kuelewa mfano huu, fikiri jinsi ilivyo ngumu kwa wewe kuelewa mifano mingine"

Mkulima anayepanda mbegu zake

"Mkulima anayepanda mbegu zake huwakilisha"

kwa yule anayepanda neno

"Neno" huwakilisha ujumbe wa Mungu. Kupanda ujumbe huwakilisha kufundisha. "yule anayefundisha watu ujumbe wa Mungu"

Baadhi huanguka kandokando mwa njia

"Baadhi ya watu ni kama mbegu huanguka kandokando mwa njia" au "Baadhi ya watu ni kama njia ya miguu ambapo mbegu huangukia"

njia

"njia ya miguu"

wanapoisikia

Hapa wanapo-"i" sikia urejea "neno" au "ujumbe wa Mungu"

Mark 4:16

Na baadhi ni wale

"Na baadhi ya watu ni kama mbegu." Yesu anaanza kuelezea ni kwa namna gani wanafanana kama mbegu zinazoangukia udongo wa mawe.

Na hawana mizizi yoyote ndani yao

Hii ni ulinganishi wa mimea midogo kuwa inakuwa na mizizi mifupi. Mfano huu humaanisha kwamba watu kwa mara kwanza husimumika pindi wapokeapo neno, lakini hawakujitoa kwa nguvu kwalo. "Nao wanakuwa kama miche midogo isiyokuwa na mizizi"

hakuna mzizi

Hii siyo ya kutia chumvi sana katika kuelezea, tiachumvi, kusisitiza jinsi mizizi ilivyokuwa na kina kidogo.

vumilia

Katika mfano huu, "vumilia" humaanisha "kuamini" "kuendelea katika imani"

sababu ya neno

Inaweza kuwa msaada kueleza kwanini taabu huja. Ilikuja kwa sababu watu waliliamini neno. "sababu waliliamini neno"

walijikwaa

Katika mfano huu, "kujikwaa" humaanisha "kuacha kuamini ujumbe wa Mungu"

Mark 4:18

Na wengine ni wale waliopandwa katika miiba

Yesu anaanza kueleza kwa namna gani watu wanakuwa kama mbegu zinazoanguka kwenye miiba. "Na watu wengine wanakuwa kama mbegu zilizopandwa katika miiba"

wanaujali ulimwengu

"masumbufu ya maisha" au "mambo yanayo husiana na maisha ya sasa"

udanganyifu wa mali

"tamaa ya mali"

huwaingia na kulisonga neno

Kama Yesu anavyoendelea kusema kuhusu watu walio kama mbegu zinazoanguka katika ya miiba, anaeleza tamaa na masumbufu yanavyofanya kwa neno katika maisha kama miiba inavyoisonga mimea midogo.

halizai

"neno hakuna kuzaa tunda lolote katika wao"

yule aliyepanda katika udongo mzuri

Yesu anaanza kueleza namna gani baadhi ya watu wako kama mbegu zilizopandwa katika udongo mzuri. "kama mbegu zilizopandwa katika udongo mzuri"

baadhi thelathini, na baadhi sitini, na baadhi mia

Hii inarejea kwa nafaka ilitokana na mimea. "baadhi huzaa nafaka thelathini, baadhi nafaka sitini, na baadhi nafaka mia" au baadhi 30 nafaka, baadhi nafaka 60, na baadhi nafaka 100"

Mark 4:21

Yesu akawambia

"Yesu alisema na umati"

Je huwa unaleta taa ndani ya nyumba na kuiweka chini ya kikapu, au chini ya kitanda?

Swali hili linaweza kuandikwa kama sentensi. "Unaleta taa ndani ya nyumba na kuiweka chini ya kikapu, au chini ya kitanda!"

Kwa kuwa hakuna chochote kilichojificha ambacho hakitajulikana...njoo nje kweupe

Hii inaweza kusemwa kwa namna chanya. "Kwa kila kitu kilichojificha kitafanywa kujulikana, na chochote kilicho sirini kitakuwa peupe"

hakuna kilichojificha... hakuna siri

"hakuna kilichojificha... hakuna siri" Vifungu vyote vina maana ile ile. Yesu anasisitiza kwamba kila kilichojificha kitawekwa wazi.

Akiwapo mwenye masikio ya kusikia, na asikie!"

Hapa neno "kusikiliza" humaaanisha kuwa makini. "unapaswa kuwa makini kwa kila ninachosema"

Mark 4:24

Akawambia

"Yesu akawambia umati"

kwa kuwa kipimo mpimacho

maana zinazowezekana ni 1) Yesu anazungumza kipimo halisi na ukarimu kwa wengine au 2) huu mfano ambao Yesu anazungumzia wa "kuelewa" kama ilikuwa ni "kupima"

ndicho mtakachopimiwa, na itaongezwa kwenu

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "Mungu atakupima, na atakuongezea"

yeye atapokea zaid...na yule vitachukuliwa

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "kwa yeye Mungu atampa zaidi...kutoka kwake Mungu atavichukua"

Mark 4:26

Sentensi unganishi

Yesu basi anawambia watu mfano kueleza ufalme wa Mungu, ambapo kwa badae anawaeleza wanafunzi wake.

kama mtu aliyepanda mbegu

Yesu hufanananisha ufalme wa Mungu kwa mkulima anayepanda mbegu. "kama mkulima anayepanda mbegu"

Alipolala usiku na kuamka asubuhi

"Anamka asubuhi na kulala usiku"

jani

shina au kuchipuka

sikio

kichwa katika shina au sehemu ya mmea inashika tunda

mara hupeleka mundu

Hapa "mundu" ni maneno mbadala yanayosimama kwa mkulima au watu wanaotumwa na mkulima kwenda kuvuna nafaka. "mara huenda na mundu kuvuna nafaka" au "mara hutuma watu na mundu kuvuna nafaka"

mundu

ni upanga uliojikunja au ndoano iliyo na makali inatumiwa kuvunia nafaka

sababu mavuno ni tayari

Hapa maneno "ni tayari" ni lugha kwa ajili ya nafaka iliyo tayari kuvunwa. "sababu nafaka iko tayari kuvunwa"

Mark 4:30

tuufananishe ufalme wa Mungu na kitu gani, au tutumie mfano gani kuuelezea?

Yesu aliuliza swali hili kusababisha wasikilizaji wake kufikiri kuhusu ufalme wa Mungu. "Pamoja na mfano huu naweza kueleza ufalme wa Mungu ukoje"

pindi inapopandwa

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "wakati yoyote anapanda mbegu" au "wakati yoyote anapanda mmea"

inafanya matawi makubwa

Mti wa haradali unaelezwa kama unasababisha matawi kukua makubwa. "pamoja na matawi makubwa"

Mark 4:33

alisema neno kwao

Neno "kwao" urejea kwa umati

kwa kadiri walivyoweza kuelewa

"na kama waliweza kuelewa baadhi, aliendelea kuwaambia zaidi"

wakati alipokuwa peke yake,

Hii inamaanisha kuwa alikuwa mbali na umati, lakini wanafunzi bado walikuwa naye.

akawaelezea kila kitu

Hapa "kila kitu" ni kutia chumvi sana katika kueleza kitu au tia chumvi. Aliezea mifano yake yote. "alielezea mifano yake yote"

Mark 4:35

Sentensi unganishi

Kama Yesu na wanafunzi wake wanachukua mtumbwi kukwepa umati wa watu, upepo mkali wa dhoruba ukajitokeza. Wanafunzi wake wanaogopa wanapoona hata upepo na bahari unamtii Yesu.

akasema kwao

"Yesu alisema kwa wanafunzi wake"

upande wa pili

"upande wa pili wa bahari ya Galilaya" au "upande wa pili wa bahari"

upepo mkali wa dhoruba ukajitokeza

Hapa "ukajitokeza" ni lugha inayotumiwa kwa "kuanza" " upepo mkali wa dhoruba kuanza"

mtumbwi ulikuwa umejaa

Inaweza kuwa msaada kusema kwamba mtumbwi ulikuwa umejaa maji. "mtumbwi ulikuwa umejaa maji"

Mark 4:38

Yesu mwenyewe

Hapa "mwenyewe" husisitia kwamba Yesu alikuwa peke yake kwenye shetri"

shetri

Hii inakuwa mwishoni mwa mtumbwi. "shetri ya mtumbwi"

Wakamwamsha

Neno "waka" urejea kwa wanafunzi

haujali sisi tunakufa?

Wanafunzi waliuliza swali hili kuonyesha uoga wao. Swali hii linaweza kuandikwa kama sentensi. "unapaswa kuwa makini kwa kile kinachotokea, wote tunakufa"

tunaelekea kufa

Neno "tuna" inajumuisha wanafunzi na Yesu.

Amani, shwari

Haya maneno mawili yanafanana na yanatumiwa kwa kusisitiza

utulivu mkubwa

"ukimya mkubwa juu ya bahari" au utulivu mkubwa juu ya bahari"

Mark 4:40

Na akasema kwao

"Na Yesu akasema kwa wanafunzi wake"

Kwa nini mnaogopa? Je hamna imani bado?

Yesu anauliza maswali haya kuwafanya wanafunzi kufikiri kwanini wanaogopa wakati yuko pamoja nao. Haya maswali yanaweza kuandikwa kama sentensi. "Haupaswi kuogopa. Unahitaji imani zaidi"

Huyu ni nani tena, kwa sababu hata upepo na bahari vya mtii?

Wanafunzi wanauliza swali katika hali ya kushangaa kwa yale Yesu alifanya. Hili swali linaweza kuandikwa kama sentensi. "Huyu mtu si kama watu wengine wa kawaida; hata upepo na bahari unamtii!"

Mark 5

Marko 05 Maelezo ya Jumla

Changamoto za kutafsiri katika sura hii

"Talitha, koum"

Maneno "Talitha, koum" (Marko 5:41) yanatoka kwa lugha ya Kiaramu. Marko anayaandika jinsi yanavyosikika na kisha kutafsiri. (See: rc://*/ta/mtu/translate/translate-transliterate)

<< | >>

Mark 5:1

Sentensi unganishi

Baada ya Yesu kutuliza dhoruba kubwa, anamponywa mtu aliyekuwa na mapepo mengi, lakini wenyeji wa Gerasi hawakufurahi kwa uponyaji wake, na walimuomba Yesu aondoke.

Walikuja

Neno "Wali" urejea kwa Yesu na wanafunzi wake.

bahari

Hii urejea kwa Bahari ya Galilaya

Gerasenes

Hili jina urejea kwa watu wanaoishi Gerasi.

akiwa na roho chafu

Hii lugha inayomaanisha kwamba mtu "ametawaliwa" au "kumilikiwa" na roho chafu. "kutawalia na roho chafu" au roho chafu kumiliki"

Mark 5:3

Alikuwa amefungwa nyakati nyingi

Hii inaweza kuandikwa katika kauli tendaji. "Watu walimfunga mara nyingi"

viungo vyake viliharibika

Hii inaweza kuandikwa katika kauli tendaji. "kuharibika kwa viungo vyake"

Viungo

"kamba kwenye miguu yake" au "minyororo iliyofungwa kifundoni kumzuia"

minyororo

"pingu" au "minyororo ilifungwa kwenye kifundo cha mkono kumzuia"

kumshinda

"mwenye kumzuia" Mtu mwenye pepo mchafu hakuna hata mmoja aliyekuwa na nguvu za kumshinda

kumshinda

"kumtawala"

Mark 5:5

alijikata yeye mwenyewe kwa mawe makali

Mara nyingi wakati ambapo mtu anamilikiwa na pepo, pepo atamsababisha mtu huyo kufanya vitu vya uharibifu, kama vile kujikata mwenyewe.

Alipomwona Yesu kwa mbali

Wakati ambapo mtu huyu alipomwona Yesu, Yesu alikuwa anatoka mtumbwini.

kuinama

Hii inamaanisha aliinama mbele za Yesu kwa hofu na heshima, na wala si kwa kuabudu.

Mark 5:7

Akapiga kelele

"Roho chafu ikapiga kelele"

Nina nini nawe, Yesu, Mwana wa Mungu aliye juu?

Roho chafu inauliza swali hili kwa uoga. Hii inaweza kuandikwa kama sentensi. "Niache peke yangyu, Yesu, Mwana wa Mungu aliye juu! Hakuna sababu ya wewe kuniingilia mimi"

Yesu...usinitese.

Yesu, "Mwana wa Mungu aliye juu,"ana uwezo kuzitesa roho chafu.

Mwana wa Mungu aliye juu

Hiki ni cheo muhimu kwa Yesu.

Nakuombwa kwa Mungu mwenyewe

Hapa roho chafu anaapa kwa Mungu kama anafanya ombi la Yesu. Angali namna gani ya ombi hili linafanywa katika lugha ya kwenu.

Mark 5:9

Alisema kwake, "Jina langu ni Jeshi, kwa kuwa tuko wengi."

roho zilizokuwa ndani ya mtu zilisema kwa Yesu kwamba haimo roho chafu moja tu ndani ya mtu huyu, bali roho wengi wachafu.

Mark 5:11

nao walimsihi

"roho chafu walimsihi Yesu"

Aliwaruhusu

"Yesu aliziruhusu roho chafu" zikawaingie nguruwe

na walikimbilia

"na nguruwe walikimbilia"

nao walikimbilia chini ya kilima mpaka baharini, na karibia nguruwe elfu mbili walizama baharini

Unaweza kuifanya hii sentensi kujitegemea: "mpaka baharini. Kuliwakuwako na nguruwe elfu mbili, na walizama baharini."

Yapata nguruwe elfu mbili

"Yapata nguruwe 2000 " walizama baharini

Mark 5:14

katika mji na nchi

Inaweza kusemwa kwa usahihi kuwa watu walitoa taarifa yao kwa watu walikuwa katika mji na nchi.

Jeshi

Hili lilikuwa jina la mapepo mengi ambayo yalikuwa ndani mwa mtu.

katika akili yake timamu

Hii ni lugha inayoamaanisha kuwa anafikiri vizuri. "kwa akili timamu" au "kufikiri kwa usahihi.

waliogopa

Neno "wa" urejea kwa kundi la watu walioenda nje kuona nini kimetokea.

Mark 5:16

Mtu aliyekuwa akitawaliwa na mapepo

"Mtu ambaye mapepo yalimtawala"

Mark 5:18

mapepo-aliyekuwa amepagawa na mapepo

amepagawa na mapepo- Ijapokuwa mtu hajapagawa na mapepo tena, bado anaelezwa katika hali hiyo. "mtu aliyekuwa amepagawa na mapepo"

Lakini hakumruhusu

Alichofanya Yesu hakikumruhusu mtu kufanya inaweza kusema kwa usahihi. "Lakini hakumruhusu mtu kuja nao"

Dekapoli

Mkoa uliokuwa kusinimashariki mwa Bahari ya Galilaya

kila mmoja alistaajabu

Inaweza kuwa msaada kusema kwanini watu walistaajabu. "watu wote waliosikia alichosema walistaajabu"

Mark 5:21

Sentensi unganishi

Baada ya kumponya mtu aliyemilikiwa na pepo katika mji wa Gerasenes, Yesu na wanafunzi wake wanarudi kupitia ziwa Kaperinaumu ambapo mmoja wa watawala wa sinagogi anamuuliza Yesu kumponya binti yake.

upande mwingine

Inaweza kuwa msaada kuongoza taarifa kwa maneno haya. "upande wa pili wa bahari"

kando mwa bahari

"ufukoni mwa bahari" au "katika ufuko"

bahari

Hili ni bahari la Galilaya.

Yairo

Hili ni jina la mwanaume.

Kwa hiyo alienda kwake

"Hivyo Yesu alienda pamoja na Yairo." Wanafunzi wa Yesu walienda pia naye. "Hivyo Yesu na wanafunzi walienda na Yairo"

weka mikono yako

"Kuweka mikono" urejea kwa nabii au mwalimu kuweka mkono wake kwa mtu na kugawa aidha uponyaji au baraka. Katika jambo hili, Yairo anamuomba Yesu kumponya binti yake.

kwamba afanywe mzima na aishi

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "na mponye na kumfanya hai"

na walimzonga karibu wakimzunguka.

Hii inamaanisha umati walimzunguka Yesu na kujisonga wenyewe kuwa karibu na Yesu.

Mark 5:25

Sentensi unganishi

Wakati Yesu akiwa katika njia kumponya mtoto wa miaka 12 wa mtu mmoja, mwanamke aliyekuwa anaumwa miaka 12 anaingilia kati kwa kumgusa Yesu kwa ajili ya uponyaji.

Sasa kulikuwa na mwanamke

"Sasa" inaonyesha kuwa huyu mwanamke ambaye ametambulishwa kwa simulizi katika lugha yako.

ambaye damu yake ilitoka kwa muda miaka kuma miwili

Mwanamke hakuwa na kidonda kilichokuwa wazi; badala yake, kutokwa kwa damu yake kwa kila mwezi hakukukoma. Lugha yako inaweza kuwa na njia ya heshima kurejea kwa hali hii.

kwa miaka kumi na miwili

"kwa miaka 12"

alikuwa vibaya

"ugonjwa wake ilikuwa mbaya" au "kutokwa damu kuliongezeka"

taarifa kuhusu Yesu

Alikuwa amesikia taarifa kuhusu Yesu kwa jinsi alivyoponya watu. " Kuwa Yesu aliponya watu"

vazi

vazi la nje au mkoti

Mark 5:28

nitakuwa mzima

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "itaniponywa mimi" au "nguvu yake itaniponywa mimi"

aliponywa kutoka kwenye mateso yake.

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "ugonjwa ulimwacha" au " hakuwa tena na ugonjwa"

Mark 5:30

na unasema, 'Ni nani aliyenigusa?'

"tulishangaa kusikia ukisema kwamba mtu fulani alikugusa."

umati huu ulimsonga

Hii inamaanisha walimsonga Yesu na kusukuma wenyewe kwa pamoja kuwa karibu na Yesu.

Mark 5:33

alianguka chini mbele yake

"alipiga magoti mbele zake." Alipiga magoti mbele ya Yesu kama tendo la heshima na utii.

kumwambia ukweli wote

Maneno "ukweli wote" urejea kwa namna alivyomgusa na kupona. "kumwambia ukweli wote kuhusu alivyomgusa"

Binti

Yesu alikuwa akiitumia istilahi hii kwa mfano kurejea kwa mwanamke kama muumini.

imani yako

"imani yako kwangu"

Mark 5:35

Wakati alipokuwa akiongea

"Wakati Yesu alipokuwa akizungumza"

baadhi ya watu walikuja kutoka kwa kiongozi wa Sinagogi

Maana zinazowekana ni 1) watu hawa walitokea nyumbani mwa Jarius au 2) Jarius alikuwa amewapa watu hawa maagizo kwenda kumuona Yesu au 3) watu hawa walikuwa wametumwa na mtu aliyekuwa kama mwenyekiti na kiongozi wa Sinagogi kwa kukosekana kwa Jarius.

kiongozi wa Sinagogi

"kiongozi wa Sinagogi" ni Jarius

kuzungumza

"kuzungumza na Jairus

Kwa nini kuendelea kumsumbua mwalimu zaidi?

"Hatupaswi kumsumbua mwalimu zaidi"

mwalimu

Hii inarejea kwa Yesu

Mark 5:36

Amini tu

Kama ni muhimu, unaweza kusema kuwa Yesu anamuamru Jarius kuamini. "Amini tu naweza kumfanya binti yako kuwa hai"

hakuwa...aliona

Katika mistari hii neno "a" urejea kwa Yesu.

kuongozana naye

"kwenda naye" Inaweza kuwa msaada kusema wakati walipokuwa wakienda. "kuongozana naye kwa nyumba ya Jarius"

Mark 5:39

aliwaambia

"Yesu aliwaambia watu walikuwa wakilia"

Kwa nini mnafadhaika na kwa nini mnalia?

Yesu aliuliza swali hili kuwasaidia kuona imani yao ndogo. Hii inaweza kuandikwa kama sentensi "Hampaswi kufadhaika na kulia."

aliwatoa wote nje

"watoe watu wengine wote nje ya nyumba"

wale waliokuwa pamoja naye

Hii inarejea kwa Petro, Yakobo, na Yohana

alienda alipokuwa mtoto

Inaweza kuwa msaada kusema alipokuwa mtoto. "alienda chumbani pale alipokuwa amelala mtoto."

Mark 5:41

Talitha koum

Hii ni sentensi ya kiaramu, ambayo Yesu alimwambiaa binti katika lugha yake.

Alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili

"alikuwa na miaka 12"

Aliwaamuru kwa nguvu kwamba hakuna yeyote anapaswa kujua kuhusu hili

"Aliwaamuru kwa nguvu, hakuna yeyote anapaswa kujua hili" au "Aliwaamuru kwa nguvu, Wasimwambie yeyote kuhusu aliyoyafanya!"

Aliwaamuru kwa nguvu

"Aliwaamuru kwa nguvu"

Na aliwaambia wampatie yule binti chakula

Na aliwaambia, 'mpeni chochote ale"

Mark 6

Marko 06 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

"Watiwa mafuta"

Katika inchi ya Mashariki ya Karibu wakati wa kale, watu walijaribu kuponyesha wagonjwa kwa kuwawekea mafuta ya mizeituni.

<< | >>

Mark 6:1

Sentensi unganishi

Yesu anarudi kwa mji wa nyumbani ambapo anakataliwa.

mji wake wa nyumbani

Hii inarejea kwa mji wa Nazarethi ambao Yesu alikulia na familia yake inaishi. Hii hana maana ya kuwa anamiliki ardhi.

Ni hekina gani aliyopewa?

Hili swali, ambalo lina muundo wa tulivu, inaweza kuulizwa katika kauli tendaji. "Hii ni hekima ya namna gani aliyopata?"

kwamba anafanya kwa mikono yake

Haya maneno yanasisitiza kuwa Yesu mwenyewe anafanya miujiza.

Huyu si seremala, kijana wa Mariamu, na ndugu yake Yohana na Yose na Yuda na Simoni? Dada zake zake hawapo hapa kati yatu?

Si huyu ni seremala, kijana wa Mariamu, na kaka yake Yohana na Yose na Yuda na Simoni? Dada zake hawapo hapa kati yetu?

Mark 6:4

kwao

"kwa umati"

Nabii hakosi heshima ila

Ni hakika kabisa kwamba wananiheshimu na manabii wengine wa sehemu nyingine,lakini si ndani ya miji tuliozaliwa! Hata kidogo na watu wanaoishi katika nyumba zetu hawatuheshimu!"

aliwawekea mikono wagonjwa wachache

"kuwawekea mikono" inarejea kwa nabii au mwalimu kuweka mikono yake kwa yeyote na kutoa aidha uponyaji au baraka. Katika jambo hili, Yesu anaponya watu.

Mark 6:7

Sentensi unganishi

Yesu anatuma wanafunzi wake nje wawili wawili kuhubiri na kuponya.

aliwaita kumi na wawili

Hapa neno "aliwaita" linamaanisha kuwa aliwaita kumi na wawili waje kwake.

Wawili wawili

" 2 kwa 2" au "jozi" msivae kanzu mbili msichukue shuka nyingine."

hapana mkate

Hapa "mkate" ni neno yenye maana sawa na chakula kwa ujumla.

hapana pesa katika mkoba

Katika utamaduni, wanaume walibeba pesa zilizowekwa katika mkanda. "hapana pesa iliwekwa kwenye mfuko wa pesa"

Mark 6:10

akawaambia

"Yesu akawaambia kumi na wawili"

kaeni hapo mpaka mtakapoondoka

"kaeni katika nyumba ile mpaka mtakapoondoka katika mji ule."

kama ushuhuda kwao

"kama ushuhuda kinyume nao." Inaweza kuwa msaada kueleza namna hili tendo lilikuwa ushuhuda kwao. "kama ushuhuda kwao. Kwa kufanya hivyo, utaweza kushuhudiwa kuwa hawakuwakaribisha"

Mark 6:12

Nao wakaenda

Neno "waka" urejea kwa kumi na wawili na haimjumuishi Yesu. Pia, inaweza kuwa msaada kusema kwamba walienda katika miji baadhi. "

kuacha dhambi zao

"tubu dhambi zao"

Waliwafukuza pepo wengi

Inaweza kuwa msaada kusema kwamba walifukuza pepo nje ya watu. "Walifukuza pepo wengi nje ya watu"

Mark 6:14

Sentensi unganishi

Wakati Herode anasikia kuhusu miujiza ya Yesu, anakuwa na wasiwasi, kufikiri kwamba mtu fulani amemfufua Yohana Mbatizaji kutoka kwa wafu. (Herode alisababisha Yohana Mbatizaji kuuwawa.)

Mfalme Herode aliposikia hayo

Neno "hayo" urejea kwa kila kitu ambacho Yesu na wanafunzi wake walikuwa wakifanya katika miji baadhi, ikiwemo na kukemea mapepo na kuponywa watu.

Baadhi walikuwa wakisema, "Yohana mbatizaji

Baadhi ya watu walikuwa wakisema kuwa Yesu alikuwa ni Yohana Mbatizaji. Hii inaweza kusemwa kwa uwazi zaidi. "Baadhi yao walikuwa wakisema, 'Ni Yohana Mbatizaji alie rejea"

Yohana mbatizaji amefufuliwa

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "Mungu alimfufua Yohana Mbatizaji"

Baadhi yao wakasema, "Huyu ni Eliya."

Inaweza kuwa msaada kusema kwanini baadhi ya watu walifikiri kuwa ni Eliya. "Baadhi wao walisema, ni Eliya, ambaye Mungu aliahidi kumtuma tena."

Mark 6:16

Maelezo ya ujumla

Katika mstari wa 17 mwandishi anaanza na kutoa maelezo ya nyuma kuhusu Herode na kwanini alimkata kichwa Yohana Mbatizaji.

yupi alimkata kichwa

Hapa Herode anatumia neno "Ni" ikirejea kwake mwenyewe. Neno "Ni" mbadala linalotumika kwa maaskari wa Herode. "ambao niliamuru maaskari wangu kumkata kichwa."

amefufuliwa

Hiii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "amekuwa hai tena"

Herode aliagiza Yohana akamatwe na alimfunga gerezani

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "Herode alituma maaskari wake kumshika Yohana na kumfunga gerezani"

kutumwa kumshika

"amri ya kumshika"

kwa ajili ya Herode

"kwa sababu ya Herode"

ndugu wa mke wa Filipi

"mke wa ndugu yake Filipo." Ndugu wa Herode ambaye ni Filipo siyo sawa na Filipi ambaye alikuwa mwinjilisti katika kitabu cha Matendo ya mitume aur Filipi aliyekuwa mmoja wa wanafunzi wa Yesu.

kwa sababu alikuwa amemuoa

"kwa sababu Herode alikuwa amemuoa"

Mark 6:18

alitaka kumuua, lakini hakuweza

Binti wa Herode ni mtendaji mkuu katika kifungu hiki na "binti" ni maneno mbadala kama anavyotaka mtu fulani amuuwe Yohana. "alitaka mtu fulani amuuwe, lakini asinge muuwa"

maana Herode alimwongopa; alimjua

Hivi vifungu viwili vinaweza kuunganishwa tofauti kuonyesha zaidi kwanini Herode alimwogopa Yohana. "maana Herode alimwogopa Yohana kwa sababu alimjua"

alijua kwamba ni mwema

"Herode alimjua kuwa Yohana alikuwa mwema"

Msikilize yeye

"Msikilize Yohana"

Mark 6:21

Sentensi unganishi

Mwandishi anaendelea kutoa maelezo ya nyumba kuhusu Herode na kukatwa kichwa Yohana mbatizaji.

akawaandalia moafisa wake karamu... Galilaya

Hapa neno "aka" urejea kwa Herode na maneno mbadala kwa mtumwa wake ambaye angeweza kumwamuru kuandaa karamu. " alikuwa na chakula kilichokuwa kimaandaliwa kwa ajili ya maofisa... wa Galilaya" au alikuwa amealika maofisa wake... wa Galilaya kuwa na kufurahi pamoja naye"

Chakula

chakula cha kawaida au dhifa

Binti wake mwenyewe Herode

Neno "wake mwenyewe"ni nomino inayotumiwa kusisitiza kwamba ilikuwa ni muhimu alikuwa ni binti wake Herode aliye cheza wakati wa karamu.

alikuja ndani

"alikuja ndani ya chumba"

Mark 6:23

chochote utakachoniomba...ufalme wangu

Hii inaweza kuwa msaada kuongeza maelezo yanayokosekana. "Nitakupa nusu ya kile ninachomiliki na kutawala, kama utaniomba"

akatoka nje

"akatoka nje ya chumba"

mara moja

"sasa hivi"

ndani ya sahani

juu ya kisahani

Mark 6:26

kwa sababu ya kiapo chake, na kwa wageni wake

"kwa sababu ya wageni wake waliosikia akitoa ahadi,"

juu ya sahani

"juu ya kisahani"

Na wanafunzi wake

"Na wanafunzi wa Yohana"

Mark 6:30

Sentensi unganishi

Baada ya wanafunzi kurudi toka kuhubiri na kuponya, wanaenda sehemu nyingine kuwa na faragha, lakini kuna watu wengi wanakuja kumsikiliza Yesu anafundisha. Wakati ambapo kunakuwa jioni, anawalisha watu na kisha anawatuma kila mmoja wakati akiomba peke yake.

eneo la jangwa

eneo ambalo halikuwa na watu

wengi walikuwa wanakuja na kwenda

Hii inamaanisha kwamba watu waliendelea kuja kwa mitume na kisha kwenda mbali nao.

hata hawakuwa

Neno "hawa" urejea kwa mitume.

Hivyo walienda zao

Hapa neno "wali" inawajumuisha mitume na Yesu.

Mark 6:33

waliwaona wakiondoka

"watu walimuona Yesu na mitume wakiondoka"

kwa miguu

Watu walienda kwa miguu kutoka miji yote, ambapo inajipinga na namna wanafunzi walienda kwa mtumbwi.

aliona umati mkubwa

"Yesu aliona umati mkubwa"

walikuwa kama kondoo wasiokuwa na mchungaji

Yesu analinganisha watu kwa kondoo waliochanganyikiwa pindi wanapokosa mchungaji wao wa kuwaongoza.

Mark 6:35

Muda ulipoendelea sana

Hii inamaanisha ilikuwa ni jioni. "Wakati ambapo kulikuwa kumeendelea" au " kuendelea jioni"

eneo la jangwa

Hii inarejea kwa eneo ambalo hakuna watu. Ona kama ilivyo tofasiri katika 6:30

Mark 6:37

Lakini akawajibu na akisema

"Lakini Yesu aliwajibu na akisema kwa wanafunzi wake"

Tunaweza kwenda na kununua mikate yenye thamani ya dinari mia mbili na kuwapa?

Wanafunzi wanauliza swali hili kusema kwamba hakuna njia wanaweza kununua chakula cha kutosha kwa umati huu. "Hatuwezi kununua mikate ya kutosha kulisha umati huu, hata kama tungekuwa na dinari mia mbili!"

dinari mia mbili

"200 dinari." Dinari ni sarafu za Kirumi.

mikate

"mikate" Mikate ni donge la unga lilotengenezwa na kuokwa.

Mark 6:39

nyasi za kijani

Eleza nyasi kwa rangi ya neno inavyotumika katika lugha yako kwa nyasi zenye afya, ambayo inaweza ua isiwe rangi ya kijani.

makundi ya mamia na hamsini

Hii urejea kwa namba ya watu katika kila kundi. "wapatao watu hamsini katika baadhi ya makundi na wapatao watu mia kwa makundi mengine"

kutazama mbinguni

Hii inamaanisha kwamba alitazama juu mbinguni, ambako kunausishwa na sehemu anayoishi Mungu.

alibariki

"alizungumza baraka" au "alishukuru"

aligawa samaki wawili kwa watu wote

"aliwagawa samaki wawili ili kwamba kila moja apate kitu"

Mark 6:42

Walichukua

Maana zinazoweza ni 1) "Wanafunzi walichukua au 2) "Watu walichukua"

vipande vya mikate, vikapu kumi na viwili

"vikapu kumi na viwili vilijaa vipande vya mkate"

vikapu kumi na mbili

"12 vikapu"

wanaume elfu tano

"5,000 wanaume"

Na walikuwa wanaume elfu tano waliokula mikate

Hesabu ya wanawake na watoto haikuhesabiwa. Kama isingeelewaka kuwa wanawake na watoto walikuwapo, inaweza kuwekwa kwa usahihi. "Na kulikuwa na watu elfu tano walio kula mikate. Hawakuwahesbau wanawake na watoto"

Mark 6:45

sehemu nyingine

Hii inarejea kwa Bahari ya Galilaya.

Bethsaida

Huu ni mji uliopo pwani ya kaskazini katika bahari ya Galilaya.

Walipokuwa wamekwisha kuondoka

"Walipokuwa watu wamekwisha kuondoka"

Mark 6:48

Sentensi unganishi

Dhoruba inajitokeza wakati wanafunzi wanajaribu kuvuka ziwa. Kumuona Yesu anatembea juu ya maji kunawaogopesha. Hawaelewi namna gani Yesu anaweza kutuliza dhoruba.

kuangilia mara ya nne

Huu ni wakati kati ya saa tatu asubuhi na jua linajomoza.

Mzimu

roho ya mtu aliyekufa au aina zingine za roho

Muwe wajasiri!...Msiwe na hofu!

Sentensi hizi mbili zinafanana katika maana, zinasisitiza kwa wanafunzi kwamba hawakupaswa kuogopa.

Mark 6:51

Wakamshangaa kabisa

Kama unataka kuwa mahususi zaidi, inaweza kusemwa nini walikuwa wakishangaa. "Walishangazwa na kila alichokuwa amekifanya"

mikate ilimaanisha nini

Neno "mikate" urejea wakati Yesu alipoizidisha mikate.

mioyo yao ilikuwa migumu

Kuwa na mioyo inawakilisha kuwa wagumu kuelewa.

Mark 6:53

Sentensi unganishi

Wakati Yesu na wanafunzi wake wanafika Genesareti wakiwa katika mtumbwi wao, watu wanamuona na kumletea watu awaponye. Hii inatokea kokote waendako.

Genesareti

Hili ni jina la mkoa kaskazi mwa magharibi mwa Bahari ya Galilaya.

mara wakamtambua

"watu pale walimtambua Yesu"

walikimbia...waliposikia

Neno "wa" urejea kwa watu waliomtambua Yesu, wala si kwa wanafunzi.

wagonjwa

Neno hili urejea kwa watu. "watu wagonjwa"

Mark 6:56

Popote alipoingia

"Popote Yesu alipoingia"

waliwaweka

Hapa "wa" urejea kwa watu. Haaina maana ya kurejea kwa wanafunzi wa Yesu

mgonjwa

Hii urejea kwa watu. "watu wagonjwa"

wakamsihi

Maana zinazowekana ni 1)"mgonjwa alimsihi" au 2) "watu walimsihi"

waache waguse

Neno "wa" urejea kwa mgonjwa.

pindo la vazi lake

"pindo la vazi lake" au " pindo la vazi lake"

wengi

"wote"

Mark 7

Mark 07 General Notes

Structure and formatting

Some translations set poetry farther to the right than the rest of the text to show that it is poetry. The ULB does this with the poetry in 7:6-7, which is from the Old Testament.

Special concepts in this chapter

Hand washing

The Pharisees washed many things that were not dirty because they were trying to make God think that they were good. They washed their hands before they ate, even when their hands were not dirty, though the law of Moses did not say that they had to do it. Jesus told them that they were wrong and that people make God happy by thinking and doing the right things. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lawofmoses and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#clean)

Other possible translation difficulties in this chapter

"Ephphatha"

This is an Aramaic word. Mark wrote it the way it sounds using Greek letters and then explained what it means. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/jit.html#translate-transliterate)

<< | >>

Mark 7:1

Sentensi unganishi

Yesu anawakemea Mafarisayo na waandishi

walikusanyika kumzunguka yeye

"walikusanyika kumzunguka Yesu"

Mark 7:2

Na waliona

"na Mafarisayo na wandishi waliona"

kwa mikono najisi

Inaweza kuwa msaada kuongeza maelezo yanayokosekana. "kwamba, walikula na mikono najisi"

wazee

Wazee wa kiyahudi walikuwa viongozi katika jamii zao na pia walikuwa waamuzi wa watu.

vyombo vya shaba

"mabirika ya shaba" au "vyombo vya vyuma"

viti vinavyotumika wakati wa chakula

"benchi" au "vitanda". Kwa wakati huo, Wayahudi wange egemea kitu wakati wa kula.

Mark 7:5

Kwa nini wanafuni wako hawaishi kulingana na tamaduni za wazee, kwani wanakula mikate yao kwa mikono isiyooshwa?

"Wanafunzi wako hawatii tamaduni za wazee wetu! Wanapaswa kuosha mikono yao kwa kutumia ibada zetu!"

Mark 7:6

Maelezo ya ujumla

Hapa Yesu ananukuu kwa nabii Isaya, ambaye aliandika maandiko miaka mingi kabla.

kwa midomo yao

Hapa "midomo" ni kirai cha kuzungumza. "kwa kile wanachosema"

lakini mioyo yao iko mbali nami

Hapa "moyo" urejea kwa mawazo ya watu au hisia. Hii ni njia kusema kuwa watu hawajitoa kwa Mungu. "lakini hawanipendi kabisa"

Wananifanyia ibaada zisizo na maana

"Wananifanyia ibada zisizo na maana" au wananiabudu kwa utupu"

Mark 7:8

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuwakemea wandishi na Mafarisayo

kuacha

"kata kumfuata"

Anayesema mabaya juu ya

"Anaye laani"

kushikilia kwa wepesi

"shikiliza kwa nguvu" au "weka"

Mmeikataa amri...mtunze tamaduni zenu

Yesu anatumia sentensi za kejeli kuwakemea wasikilizaji wake kwa kuziacha amri za Mungu. "Mnafikiri mmefanya vizuri kwa jinsi mmemkataa amri za Mungu ili kwamba mtunze tamaduni zenu, lakini mlichofanya si vizuri kabisa!"

Mmeikataa

"mu uhodari kiasi gani kumkataa"

asemaye mabaya

"anaye laani"

hakika atakufa

"anapaswa kuuwawa"

'Yeye asemaye mabaya juu ya baba yake au mama yake hakika atakufa

Yeye asemaye mabaya juu ya baba yake au mama yake hakika atakufa hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "Mamlaka yanapaswa kumwadhibu kifo mtu anasema vibaya juu ya baba yake au mama"

Mark 7:11

Msaada wowote ambao mngeupokea kutoka kwangu ni hazina ya Hekalu.

Tamaduni za waandishi zilisema kwamba pindi pesa au vitu vingine vilipoahidiwa kanisani, visingetumika kwa lengo lingine lolote.

Hazina ya Hekalu

Mwandishi anataka msomaji ajue jinsi neno linavyo sikika, kwa hiyo andika hii kwakutumia alfabeti za lugha yako lisikike kama hili kwa kadri uwezavyo.

Hazina ya Hekalu

Hapa mwandishi anarejea kwa kitu fulani katika neno la Kiebrania. Hili neno linapaswa kunakiriwa kama ilivyo katika lugha yako kutumia alfabeti.

imetolewa kwa Mungu

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "Nimeitoa kwa Mungu"

hivyo haumruhusu kufanya jambo lolote kwa ajili ya baba au mama yake

Kwa kufanya hivi, Mafarisayo wanawaruhusu watu kutowapatia wazazi wao, kama wanatoa ahadi kumpa Mungu kila wangetoa kwao

bure

kualishwa au kuachana nayo

Na mambo mengi ya jinsi hiyo mnayoyafanya."

"Na mnavyofanya inaweza vitu vingine kufanana na hiki"

Mark 7:14

Sentensi unganishi

Yesu anazungumza mfano kwa umati kuwasaidia kuelewa alichokuwa akiwaambia waandishi na Mafarisayo.

Aliita

"Yesu aliita"

Nisikilizeni mimi, ninyi nyote, an mnielewe

Neno hili "Sikiliza" na "elewa" yanashabiana. Yesu anayatumia yote pamoja kusisitiza kwamba wasikilizaji wake lazima wawemakini kwa kile anachokisema.

kuelewa

Inaweza kuma msaada kusema nini Yesu anawaambia kuelewa. "jaribu kuelewa ninachoenda kukuambia"

Hakuna chochote kutoka nje ya mtu

Yesu anazungumza kuhusu anachokula mtu. Hii ni kinyume na "kile kitokacho mwa mtu"

Ni kile kimtokacho mtu

"Ni utu wa ndani" au "Ni kile mtu anachofikiri, anachosema, au dkufanya"

Mark 7:17

Sentensi unganishi

Wanafunzi bado hawajaelewa nini Yesu alichosema kwa waandishi, Mafarisayo, na umati. Yesu anaeleza maana zaidi kwa utoshelevu kwao.

Sasa

Neno hili limetumika hapa kuanzisha wazo jingine katika hadithi. Sasa Yesu yuko mbali na umati, yuko ndani na wanafunzi wake.

Bado hamjaelewa?

Yesu anatumia swali hili kueleza kukatishwa tamaa kwake kwamba hawaelewi. Hii inaweza kuelezwa kama sentensi. "Baada ya yote nimekwisha sema na kufanya, ningetegemea muelewe"

Hamuoni kwamba chochote kimuingiacho mtu hakiwezi kumchafua

Yesu anatumia swali hili kufundisha wanafunzi wake kitu fulani ambacho walipaswa kuwa wanakijua tayari. Inaweza kusemwa kama sentensi "Chochote kiingiacho...huchafua

kwa sababu hakiwezi

Hapa "haki" urejea kwa kile kimwingiacho mtu, kwamba, kila mtu anakula.

Yesu alifanya

"Yesu alitangaza"

vyakula vyote safi

Inaweza kuwa msaada kueleza kwa usahihi nini maana ya maneno haya. "vyakula vyote safi, inamaanisha kuwa watu wanaweza kula chakula chochote pasipo Mungu kumhesabia mlaji kuwa najisi

Mark 7:20

Alisema

"Yesu alisema"

Ni kile ambacho kinamtoka

Inaweza kuwa msaada kusema kwa ufasaha "kile" urejea kwa. "Ni mawazo na matendo yanayomtoka mtu."

kupenda anasa

kushindwa kutawala tamaa za mwili

yanatoka ndani

Hapa neno "ndani" huelezea moyo wa mtu. "hutoka ndani mwa moyo wa mtu" au "hutoka ndani mwa mawazo ya mtu"

Mark 7:24

Sentensi unganishi

Wakati Yesu anaenda Tiro, anamponya binti wa mwanamke wa kimataifa akiwa na imani ya ajabu.

alikuwa na roho chafu

Hii ni lugha inayomaanisha kuwa alikuwa amilikiwa na roho chafu.

Anguka chin

"piga magoti"

Mwanamke huyo alikuwa Myunani, wa kabila la Kifoeniki

Neno "sasa" utambulisha wazo jingine katika hadithi, kama ilivyo sentensi hii hutoa maelezo ya nyuma kuhusu mwanamke.

Kifoeniki

Hili ni jina la mwanamke la kitaifa. Alizaliwa mkoa wa Kifoeniki Syria.

Mark 7:27

Waache watoto kwanza washibe

"Watoto lazima wale kwanza" au "Lazima nilishe watoto kwanza."

Watoto

Wayahudi. AT: "Lazima nitumikie Wayahudu kwanza."

Mkate

Chakula

Mbwa

Watu wa mataifa

hata mbwa hula mabaki ya watoto chini ya meza.

"unaweza kunitumikia, mtu wa mataifa, katika njia ndogo hii.

Mabaki

Vipande vidogo vidogo sana ya mkate

Mark 7:29

uko huru kwenda

"unaweza kwenda sasa" au "nenda nyumbani"

Pepo ameshamtoka binti yako

Yesu amesababisha pepo mchafu kumtoka binti wa mwanamke. Hii inaweza kueleza kwa usahihi. "Nimesababisha roho mchafu kumwacha binti yako"

Mark 7:31

Alikuja kupitia

"Alisafiri kupitia"

Dikapoli

"miji kumi," kanda ya kusini mashariki ya Bahari ya Galilaya.

Nsni slikuwa kiziwi

"ambaye alikiwa hana uwezo wa kusikia"

alikwa na shida ya kuongea

"hakuweza kuongea vizuri"

Mark 7:33

Alimota nje

"Yesu alimtoa nje"

akaweka vidole vyake kwenye masikio yake

Yesu anaweka vidole kwenye masikio yake.

baada ya kutema mate, aligusa ulimi wake

Yesu anatema mate na kisha anagusa ulimi wa mwanaume.

baada ya kutema

Inaweza kuwa msaada kusema kwamba Yesu alitemea mate vidole vyake.

alitazama juu mbinguni

Hii inamaanisha kuwa alitaza juu mbinguni, ambako kunahusishwa na eneo analoishi Mungu.

Efata

Mwandishi anataka msomaji ajue jinsi neno linavyo sikika, Kwa hiyo andika hii kwa kutumia alfabeti za lugha yako na neno lisike karibu na "effatha" kwa kadri uwezavyo.

Kuvuta pumzi

akavuta pumzi kuonyesha kuwa hakuwa na furaha.

kusema naye

"alisema na mwanaume"

masikio yake yalifunguliwa

Hii inamaanisha alikuwa hawezi kusikia. "masikio yake yalifunguliwa na aliweza kusikia"

Kilichokuwa kimeshikilia ulimi wake kilitolewa.

"Yesu alikitoa kilichokuwa kimeushikilia ulimi wake" au "Yesu aliponya kilichokuwa kimemfanya asiongee vizuri"

kilichokuwa kimezuia ulimi

"kinachomzuia yeye kuongea " au "usemi wake kuwa na kikwazo"

Mark 7:36

kadri alivyowaamuru

Inaweza kuwa msaada kuongeza taarifa iliyokosekana. "kadri alivyowaamuru wasimwambie mtu yoyote."

kadri ya wingi

"kadri ya upana" au " zaidi"

hakika

"kabisa" au "mno"

kiziwi...kimya

Haya urejea kwa watu. "watu viziwi...watu wakimya" au " watu wasioweza kusikia...watu wasioweza kuongea"

Mark 8

Marko 08 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Mkate

Wakati Yesu alifanya muujiza na kulisha na mkate kwa umati mkubwa wa watu, labda walikumbuka wakati Mungu alifanya ajabu zamani akalisha watu wa Israeli jangwani.

Chachu ni kiungo kinachosababisha mkate kuwa kubwa kabla ya kuoka. Katika sura hii, Yesu anatumia chachu kama sitiari ya mambo ambayo yanabadili jinsi watu wanavyofikiri, kuzungumza, na kutenda. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

"Kizazi cha uzinzi"

Wakati Yesu aliwaita watu "kizazi cha uzinzi," alikuwa akiwaambia kuwa hawakuwa waaminifu kwa Mungu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faithful and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#peopleofgod)

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Maswali ya uhuishaji

Yesu alitumia maswali mengi yauhuishaji kama njia ya kuwafundisha wanafunzi (Marko 8:17-21) na kuwakaripia watu (Marko 8:12). (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-rquestion)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Kitendawili

Kitendawili ni taarifa ya kweli inayoonekana kuelezea kitu kisichowezekana. Yesu anatumia kitambo wakati anasema, "Yeyote anayetaka kuokoa maisha yake atayapoteza, na yeyote anayepoteza maisha yake kwa ajili yangu atayapata" (Marko 8:35-37).

<< | >>

Mark 8:1

Sentensi unganishi

Umati mkubwa ambao haukuwa na chakula ulikuwa na Yesu. Anawalisha kutumia mikate saba na samaki wachache mbele za Yesu na wanafunzi wake wakaingia ndani ya mtumbwi kwenda eneo jingine.

Katika siku hizo

Kikundi hiki cha maneno kinatumiwa kutambulisha tukio jipya katika hadithi.

sababu wameendelea kuwa pamoja nami tayari kwa siku tatu.

"kwa sababu hii ni siku ya tatu hawa watu wamekuwa pamoja nami"

wanaweza kuwa dhaifu

Maana zinazofaa ni 1) "wanaweza kupoteza fahamu kwa muda" au 2)wanaweza kuwa dhaifu"

Tutapata wapi mikate ya kutosha kuwashibisha watu hawa katika eneo hili lililoachwa?

Wanafunzi wanaonyesha mshangao kwamba Yesu angewatazamia kuweza kupata chakula cha kutosha. "Hili ni eneo la jangwa ambako hakuna eneo ambalo tunaweza kupata mikate ya kutosha kuwalizisha watu hawa!"

boflo ya mkate

Boflo ya mkate ni bonge la unga wa ngano ambalo linatengenezwa na kuokwa.

Mark 8:5

Akawauliza

"Yesu aliwauliza wanafunzi wake"

Aliuamuru umati ikae chini.

Hii inaweza kuandikwa kama dondoa ya moja kwa moja. "Yesu aliuamuru umati, 'ukae chini"

kaa chini

Tumia maneno ya lugha ya kwenu kwa namna watu wanakula kimatamaduni kama hakuna meza, aidha kwa kukaa au kujilaza.

Mark 8:7

Pia walipata

Hapa neno "wali..." linatumika kurejea kwa Yesu na wanafunzi wake.

alishukuru

"Yesu alishukuru kwa samaki"

Walikula

"Hawa watu walikula"

walikusanya

"wanafunzi walikusanya"

vipande vilivyo baki, vikapu vikubwa saba

Hii inaweza kuwa msaada kuongeza taarifa zilizokosekana. "vipande vilivyo baki vya mkate na samaki, ambavyo vilijaza vikapu saba vikubwa.

Na aliwaacha waende

Hii inaweza kuwa msaada kufafanua ambapo Yesu anawaacha waende. "Na baada ya kula, Yesu aliwaacha waende"

wakaenda katika ukanda wa Dalmanuta

Hii inaweza kuwa msaada kufafanua namna ya kwenda Dalmanuta. "walipiga mashua kupitia bahari ya Galilaya mpaka Dalmanuta"

Mark 8:11

Sentensi unganishi

Huko Dalmanuta, Yesu anakataa kuwapa Mafarisayo ishara kabla ya yeye na wanafunzi hawajaingia katika mashua na kuondoka.

Walitafuta toka kwake

"Walimuuliza"

kutoka mbinguni

Hapa "mbinguni" urejea kwa eneo ambapo Mungu anaishi, na ni maneno badala ya Mungu. "kutoka kwa Mungu"

kumjaribu yeye

Mafarisayo walimjaribu Yesu kumfanya yeye awathibitishie kuwa anatoka kwa Mungu. Baadhi ya taarifa zinaweza kuwekwa sahihi. "kuhakikisha kuwa Mungu alimtuma yeye"

hema

Hii inamaanisha kuvuta ndani na kisha kupumua.

katika roho wake

"katika yeye"

Kwa nini kizazi hiki kinatafuta ishara?

Yesu anawakaripia. Swali hili linaweza kuandikwa kama sentensi. "Kizazi hiki hakipaswi kutafuta ishara"

kizazi hiki

Wakati ambapo Yesu anazungumza juu ya "kizazi hiki", anarejea kwa watu walio ishi wakati huo. Mafarisayo hawa wanajumuishwa katika kundi hili. "wewe na watu wa kizazi hiki"

hakuna ishara itakayotolewa

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendi. "Sitatoa ishara"

aliwaacha, akaingia ndani ya mtumbwi tena

Wanafunzi wa Yesu walienda naye. Baadhi ya taarifa zinaweza kuwekwa sahihi. "aliwaacha, akaingia ndani ya mtumbwi pamoja na wanafunzi wake"

upande ule mwingine

Hii huelezea bahari ya Galilaya, ambayo inaweza kusemwa kwa ufasaha. "kwa upande mwingine wa bahari"

Mark 8:14

Sentensi unganishi

Wakati Yesu na wanafunzi wake wakiwa ndani ya mtumbwi, walikuwa na majadiliano kuhusu kuelewa kudogo kati ya Mafarisayo na Herode, ijapokuwa walikuwa wamekwisha ona ishara nyingi.

Sasa

Hili neno linatumika kuweka alama ya kutenganisha hadithi. Hapa mwandishi anasema taarifa za nyuma kuhusiana na wanafunzi kusahau kuchukua mkate.

hakuna zaidi ya mkate mmoja

Kikundi cha maneno yaliyo kinyume "hakuna zaidi" hutumiwa kusisitiza namna ya kiasi kidogo cha mkate waliokuwa nao. "mkate mmoja tu"

Kuwa macho na ujilinde

Haya maneno mawili yana maana ya kufanana na yanarudiwa hapa kwa msisitizo. Yanaweza kuanganishwa. "Kuwa macho"

chachu ya Mafarisayo na chachu ya Herode.

Hapa Yesu anazungumza kwa wanafunzi wake katika mfano ambao hawauelewi. Yesu analinganisha mafundisho ya Mafarisayo na Herode kwa chachu, lakini hauwezi kueleza hivi unavyo tofasiri sababu wanafunzi wenyewe hawakuuelewa.

Mark 8:16

Ni kwa sababu hatuna mikate

Katika sentensi hii, inaweza kuwa msaada kusema kwamba, "ni" urejea kwa kile Yesu alichokwisha sema. "Angepaswa kuwa amesema kwa sababu hatuna mikate"

hakuna mkate

Wanafunzi walikuwa na mkate mmoja, ambao haikuwa na tofauti kutokuwa na mkate kabisa. "mikate midogo kabisa"

Kwa nini mnasemezana kuhusu kutokuwa na mikate?

Hapa Yesu anawaonywa kwa ulaini wanafunzi wake kwa sababu wangeweza kuelewa alichokuwa anazungumzia. Hii inaweza kuandikwa kama sentensi. "Haupaswi kufikiri kwamba naongelea mkate halisi"

Hamjajua bado? Hamuelewi?

Maswali haya yana maana ile ile na yanatumika kwa pamoja kusisitiza kwamba hawaelewi. Hii inaweza kuandikwa kama swali moja au sentensi. "Hamjajua bado?" au "Mnapaswa kujua na kuelewa kwa sasa mambo ninayo sema na kufanya."

Mioyo yenu imekuwa miepesi?

Mfano huu urejea kwa hao hawako wazi au kuwa tayari kuelewa Yesu alimaanisha nini. Huu unaweza kuandikwa kama sentensi. "Namna gani mioyo yenu haiko wazi kuelewa ninachosema?" au "Mioyo yenu haiko tayari kuelewa."

Mark 8:18

Mna macho, hamuoni? Mna masikio, hamsikii? Hamkumbuki?

Yesu anaendelea kukemea kwa utilivu wanafunzi . Haya maswali yanaweza kuandikwa kama sentensi. "Una macho, lakini hauelewi unachokiona. Una masikio, lakini hauelewi unachosikia. Lazima ukumbuke"

elfu tano

Hii urejea kwa watu 5,000 Yesu aliye walisha

mlichukua vikapu vingapi vilivyo jaa vipande vya mikate?

Hii inaweza kuwa msaada kusema wakati ambapo walichukua vipande vya vikapu. "ni vikapu vingapi vilivyo jaa vipande vya mikate mlichukua baada ya kila mmoja amemaliza kula"

Mark 8:20

elfu nne

Hii urejea kwa watu 4,000 waliolishwa na Yesu.

mlichukua vikapu vingapi

Hii inaweza kuwa msaada kusema wakati ambapo walivichukua. "ni vikapu vingapi vilivyo jaa vipande vya mikate mlichukua baada ya kila mmoja amemaliza kula"

Bado hamuelewi?

Yesu kwa utilivu anawakamea wanafunzi wake kwa kushindwa kuelewa. Hii inaweza kuandikwa kama sentensi. "Lazima uelewe kwa sasa mambo ninayo sema na kufanya."

Mark 8:22

Sentensi unganishi

Wakati ambapo Yesu na wanafunzi wake wanatoka katika mtumbwi wao hukpo Bethsaida, Yesu anamponya mtu kipofu.

Bethsaida

Huu ulikuwa ni mji kaskazini mwa ufuko wa bahari ya Galilaya.

akamshika

Hii inaweza kuwa msaada kusema kwa nini walitaka Yesu amguse mtu huyo. "kumgusa ili kumponya"

Alipotema mate juu ya macho yake ...alimuuliza

"Wakati ambapo Yesu alipotema mate juu ya macho yake... Yesu alimuuliza"

Mark 8:24

Alitazama juu

"Mtu alitazama juu"

Naona watu wanaonekana kama miti inatembea

Mtu anaona watu wanatembea, na bado hawakuwa vizuri kwake, hivyo aliwalinganisha na miti. "Ndiyo, naona watu! Wanatembea, lakini siwaoni vizuri . Wanaonekana kama miti"

Kisha tena

"Yesu tena"

na mtu alifungua macho yake, macho yake yaliona

Kikundi hiki cha maneno "macho yaliona" inaweza kuandikwa katika kauli tendi "Kurudisha uonaji, na mtu akafungua macho yake"

Mark 8:27

Sentensi unganishi

Yesu na wanafunzi wake wakiwa njiani kwenda vijiji vya Kaiseria ya Filipi wanazungumza juu ya Yesu ni nani na nini kitatokea kwake.

Wakamjibu na wakasema

"Wakamjibu, wakasema,"

Yohana mbatizaji

Hili lilikuwa jibu la mwanafunzi, ambalo watu walisema Yesu alikuwa nani. Hii inaweza kuonyeshwa kwa usahihi. "Baadhi ya watu wanasema wewe ni Yohana mbatizaji"

Wengine wanasema

Neno "wengine" urejea kwa watu wengine. Pia, inaweza kuwa msaada kuongeza taarifa zinazokosekana. "Watu wengine wanasema wewe ni ... watu wengine wanasema wewe ni"

Mark 8:29

Akawauliza

"Yesu akawauliza wanafunzi wake"

Yesu akawaonya wasimwabie mtu yeyote kumuhusu Yeye.

Yesu hakutaka wao wasimwambie mtu yeyote kwamba yeye ni Kristo. Hii inaweza kufanywa kwa usahihi. Pia, hii inaweza kuandikwa kama dondoo ya moja kwa moja. "Yesu aliwaonya wasimwambie mtu yeyote kuwa ye ni Kristo" au " Yesu aliwaonya, 'msimwambie mtu yeyote kwamba mimi ni Kristo"

Mark 8:31

Mwana wa Adamu

Hili ni jina muhimu sana kwa Yesu.

na atakataliwa na viongozi na makuhani wakuu, na waandishi, na atauawa, na baada ya siku tatu atafufuka.

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendi. "na kwamba viongozi na makuhani wakuu na waandishi watamkataa, na watu hao watamuua na baada ya siku tatu atafufuka."

Alisema haya kwa uwazi

"Alisema hivi ili iwe nyepesi kuelewa"

alianza kumkemea

Petro alikemewa na Yesu kwa kusema mambo aliyosema kuwa yangetokea kwa Mwana wa Adamu. Hii inaweza kufanywa kwa usahihi. "alianza kumkemea kwa kusema mambo haya"

Mark 8:33

Sentensi unganishi

Baada ya kumkemea Petro kwa sababu hakutaka Yesu kufa na kufufuka, Yesu anawambia wanafunzi wake na umati namna ya kumfata.

Pita nyuma yangu Shetani! Hujali

Yesu anamaanisha ya kuwa Petro anafanya kama Shetani kwa sababu anajaribu kumzuia Yesu kutimiza alichotumwa na Mungu kufanya. "Pita nyuma Shetani! Nakuita Shetani kwa sababu hujali" au "Pita nyuma yangu, kwa sababu unafanya kama Shetani! Hujali"

Pita nyuma yangu

"Nipishe mimi"

nifuate mimi

Kumfuata Yesu hapa kunawakilisha kuwa mmoja wa wanafunzi wake. "kuwa mwanafunzi" au "kuwa mmoja wa wanafunzi wangu"

ajikane mwenyewe

"hawapaswi kuzitimiza tamaa zake" au "anapaswa kuziacha tamaa zake"

achukue msalaba wake, na anifuate.

"beba msalaba wake na umfuate" Msalaba huu unawakilisha mateso na kifo. Kuchukua msalaba huwakilisha kuwa tayari kutesa na kufa. "unapaswa kunitii mpaka hatua ya kuteseka na kufa"

na nifuate

Kumfuata Yesu hapa uwakilisha kumtii. "na nitii mimi"

Mark 8:35

Kwa kuwa yeyote anayetaka

"Kwa kuwa yeyote anayetaka"

maisha

Hii urejea kwa vyote maisha ya mwili na maisha ya kiroho.

kwa ajli yangu na kwa ajli ya injili

"kwa sababu yangu na kwa sababu ya injili." Yesu anazumguza juu ya watu wanaopteza maish yao kwa ajili ya kumfuata Yesu na injili. Hii inaweza kusema kwa usahihi. "kwa sababu ananifuata mimi na kuwambia wengine injili"

Inamfaidia nini mtu, kupata ulimwengu wote, na kisha kupata hasara ya maisha yake?

Hii inaweza kuandikwa kama sentensi. "Hata kama mtu anapata ulimwengu wote, haitamfaidi kama atapata hasara ya maisha yake"

kupata ulimwengu wote

Yesu anatumia kutia chumvi sana katika kusisitiza kwamba hakuna chochote ulimwenguni unachoweza kupata kwa kupoteza maisha yako. "kama anapata kila kitu katika ulimwengu"

kupoteza

"kupoteza"

Mtu anaweza kutoa nini badala ya maisha yake?

Hii inaweza kuandikwa kama sentensi. "Hakuna chochote mtu anaweza kufanya kutoa badala ya maisha yake." au " Hakuna yoyote anaweza kutoa chochote kwa badala ya maisha yake."

Mtu anaweza kutoa nini

Kama katika lugha yako "kutoa" huitaji mtu kupokea alichopewa, "Mungu" inaweza kusemwa kama mpokeaji. "Nini mtu anaweza kumpa Mungu"

Mark 8:38

Katika kizazi hiki cha zinaa na dhambi

Yesu anazungumza juu ya kizazi hiki kama "wazizi" akimaanisha kwamba si waaminifu katika mahusiano yao na Mungu. "katika kizazi hiki cha watu waliojiingiza katika uzizi kinyume na Mungu na niwazinifu" au "katika kizazi hiki cha watu wasio waaminifu kwa Mungu na ni wenye dhambi"

Mwana wa Adamu

Hili ni jina la muhimu sana kwa Yesu

atakapokuja

"atakapokuja tena"

katika utukufu wa Baba yake

Wakati ambapo Yesu anakuja atakuwa na utukufu ule ule kama wa Baba yake

pamoja na malaika watakatifu

"atafuatana na malaika watakatifu"

Mark 9

Marko 09 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

"kugeuka sura"

Maandiko mara nyingi huzungumzia utukufu wa Mungu kama mwanga mkubwa, wenye nguvu. Watu wanapoona mwanga huu, wanaogopa. Marko anasema katika sura hii kwamba mavazi ya Yesu yalikuwa na mwanga huu wa utukufu kiasi cha kuwawezesha wafuasi wake kuona kwamba Yesu kweli alikuwa Mwana wa Mungu. Wakati huo huo, Mungu aliwaambia kwamba Yesu alikuwa Mwana wake. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#glory and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#fear)

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Neno la kukaza ukweli la kupita ukweli

Yesu alisema mambo ambayo hakutarajia wafuasi wake kuelewa kwa kweli. Wakati aliposema, "Ikiwa mkono wako unakukosesha, uukate" (Marko 9:43), alikuwa akizidisha sana ili waweze kujua kwamba wanapaswa kuacha mbali na chochote kilichowaanya kutenda dhambi, hata kama ni kitu walipenda au walidhani walihitaji.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Eliya na Musa

Eliya na Musa ghafla wanaonekana kwa Yesu, Yakobo, Yohana, na Petro, na kisha kutoweka. Wote wanne waliona Eliya na Musa, na kwa sababu Eliya na Musa walizungumza na Yesu, msomaji anapaswa kuelewa kwamba Eliya na Musa walionekana kimwili.

"Mwana wa Binadamu"

Yesu anajiita mwenyewe "Mwana wa Binadamu" katika sura hii (Marko 9:31). Lugha yako huenda haiwezi kuwaruhusu watu kujizungumzia wenyewe kana kwamba wanaongea juu ya mtu mwingine. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sonofman and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-123person)

Kitendawili

Kitendawili ni taarifa ya kweli inayoonekana kuelezea kitu kisichowezekana. Yesu anatumia kitendawili wakati anasema, "Ikiwa mtu anataka kuwa wa kwanza, lazima awe wa mwisho na mtumishi wa wote" (Marko 9:35).

<< | >>

Mark 9:1

Sentensi unganishi

Yesu amekuwa akizungumza kwa watu na wanafunzi wake kuhusu kumfuata. Siku sita badae, Yesu anaenda na wanafunzi watatu juu ya mlima pale alipobadilika, kwa hiyo anaonekana kama siku moja atakavyokuwa katika ufalme wa Mungu.

Na aliwaambia

"Na Yesu aliwaambia wanafunzi wake"

ufalme wa Mungu unakuja na nguvu

Ufalme wa Mungu unakuja kumwakilisha Mungu akijionyesha yeye kama mfalme. "Mungu anajionyesha yeye mwenyewe na nguvu kuu kama mfalme"

peke yao

Mwandishi anatumia "yao" hapa kusisitiza kuwa walikuwa wao wenyewe na kwamba Yesu tu, Petro, Yakobo na Yohana welienda mlimani.

alianza kubadilika

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "alionekana tofauti sana"

kabla yao

"mbele yao"

kung'aa sana

"kung'aa" au "inang'aa" Mavazi ya Yesu yalikuwa meupe yakitoa mwanga.

kubwa

"sana, sana"

meupe zaidi, meupe kuliko mng'arishaji yeyote duniani.

Kupausha kunaelezea mchakato wa kufanya pamba nyeupe ya kiasilia zaidi ya weupe kwa kutumia kemikali ya kupausha au amonia.

Mark 9:4

Eliya na Musa

Inaweza kuwa msaada kusema hawa wanaume ni "manabii wawili walio ishi muda kitambo, Musa na Eliya."

walikuwa wakiongea

Neno "wa" urejea kwa Eliya na Musa

Petro alimjibu na kumwambia Yesu

"Petro alimwambia Yesu." Hapa neno "alimjibu" linatumiwa kumtambulisha Petro katika mazungumzo. Petro alikuwa hajibu swali.

sisi

Hili neno urejea kwa Petro, Yakobo, na Yohana

vibanda

"mahema" Hii urejea kwa makao rahisi ya muda.

Kwa kuwa hakujua nini cha kusema, waliogopa sana

Sentensi hii iliyo kwenye mabano usema maelezo ya nyuma kuhusu Petro, Yakobo, na Yohana.

ogopa

kuogopa sana

Mark 9:7

wingu lilitokea na kuwafunika

"kutokea na kuwafunika"

Ndipo sauti ikatoka mawinguni

"Sauti" ni kirai cha Mungu. Pia, "sauti" inaelezwa kama "inatoka mawinguni", ikimaanisha kuwa walimsikia Mungu akuzungumza kutoka mawinguni. "Kisha Mungu alizungumza toka mawinguni"

Huyu ni mwanangu mpendwa. Msikieni

Mungu Baba aliezea upendo wake kwa mwanae mpendwa, Mwana wa Mungu.

Mwana mpendwa

Hili ni jina muhimu kwa Yesu.Mwana wa Mungu.

walipokuwa wakitazama

Hapa "wa" urejea kwa Petro, Yakobo, na Yohana.

Mark 9:9

aliwaamuru kutokumwambia mtu yeyote yale yote waliyoyaona, mpaka Mwana wa Adamu atakapofufuka kutoka kwa wafu.

Hii inamaanisha kuwa alikuwa akiwaruhusu wawaambie watu kuhusu kile walichokiona tu baada ya kufufuka kutoka kwa wafu.

Kufufuka kutoka kwa wafu

"Kuwa unaishi tena baada ya kufa"

Waliyatunza mambo wao wenyewe.

"Hivyo hawakusema kuhusu mambo haya kwa yeyote ambaye hakuyaona pia yaliyotokea.

Mark 9:11

Eliya afanya kweli...watu watamchukia yeye?

Ijapokuwa Petro, Yakobo, na Yohana walishangaa nini Yesu angemaanisha na "kufufuka toka kwa wafu," walimuuliza badala ya ujio wa Eliya.

Walimuuliza

Neno "wa" urejea kwa Petor, Yakobo, na Yojhana.

Kwa nini waandishi wanasema kuwa Eliya anapaswa kuwa kwanza?

Unabii unasemswa kwamba Elijah ambaye angekuja toka mbinguni. Kisha Masihi, ambaye ni Mwana wa Adamu, atakuja kutawala na Mwana wa Adamu atakuja kuteseka na kuchukiwa na watu. Wanafunzi wamechanganyikiwa ni kwa namna gani hivi viiwili vinaweza kweli.

kwamba Eliya anapaswa kuja wa kwanza

Waandishi walifundisha kuwa Eliya angerudi tena ulimwenguni kabla ya Masihi kuja.

Kwa nini imeandikwa...achukiwe

Kama Yesu anafundisha wanafunzi wake, anauliza swali hili na kisha kuwaambia wanafunzi wake jibu. Hii inaweza kama sentensi. "Lakini pia nataka wewe ufikirie kile kilichoandikwa kuhusu Mwana wa Adamu. Maandiko yanasema kuwa anapaswa kuteseka kwa mambo mengi na kufanyiwa vibaya kama aliyechukiwa"

apate mateso mengi na achukiwe?

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "na watu walimtenda kama mtu aliyechukiwa"

na walimfanya kama walivyopenda

Inaweza kuwa msaada kusema nini watu walimfanya kwake. "na viongozi wetu walimfanyia vibaya, kama jinsi walivyo taka kufanya"

Mark 9:14

Sentensi unganishi

Wakati Petro, Yakobo, Yohana na Yesu walipokuja chini kutoka mlimani, waliwakuta waandishi wakibishana na wale wanafunzi wengine.

walirudi kwa wanafunzi

Yesu, Petro, Yakobo na Yohana walirudi kwa wanafunzi wengine ambao hawakuenda nao mlimani.

waandishi walikuwa wakibishana

Waandishi walikuwa wakibishana na wanafunzi ambao hawakuenda pamoja na Yesu.

linashangaa

Inaweza kuwa msaada kusema kwanini walishangaa. "walishangaa kwa kuwa Yesu alikuwa amekuja"

Mark 9:17

Sentensi unganishi

Kueleza nini waandishi na wale wanafunzi walikuwa wakibishania nini, baba wa yule kijana aliye na mapepo anamwambia Yesu kwamba amewauliza wanafunzi kutoa pepo kwa kijana, lakini hawakuweza. Yesu kisha analitoa pepo nje ya mvulana. Baadaye wanafunzi wanauliza kwa nini halishindwa kumtoa pepo.

Ana roho

Hii inamaanisha yule kijana ana roho chafu. "Ana roho chafu"

kutoka povu mdomoni

Wakati mtu anakuwa na mshtuko, wanaweza kuwa na shida ya kupumua au kuvuta hewa. Hii inasababisha kutoka povu mdomoni. Kama lugha yako ina njia kueleza hili, unaweza tumia.

anakuwa mgumu

"kuwa mwenye shingo ngumu" Inaweza kuwa msaada kusema kwamba ni mwili wake unaokuwa mgumu.

hawakuweza

Inaweza kuwa msaada kuongeza maelezo yaliyokosekana. "hawakuweza kutoa roho chafu nje yake"

Aliwajibu

Ijapokuwa alikuwa ni baba wa kijana aliyefanya ombi kwa Yesu, Yesu anaitikia kwa umati wote. Hii inaweza kusemwa kwa usahihi. "Yesu aliitikia kwa umati"

Kizazi cha wasioamini

"Nyie kizazi cha wasioamini" Yesu anaita umati wake hivi, kama anavyoanza kuwajibu.

nitakaa nanyi kwa muda gani?...nitachukuliana nanyi

Yesu anatumia maswali haya kueleza kukatishwa tamaa kwake. Yote maswali yana maana ile ile. Yanaweza kuandikwa kama sentensi. " Nimechoshwa na kutoamini kwenu!" au "Kutoamini kwenu kumenichosha! Nashangaa kwa muda gani nitachukuliana nanyi."

Nitachukuliana nanyi

"nitachukuliwana nanyi" au "kuvumialiana nanyi"

Mleteni kwangu

"Mleteni mvulana kwangu"

Mark 9:20

roho

Hii urejea kwa roho chafu.

tetemeko

Hii ni hali ambayo mtu hana wa uwezo wa kujiongoza juu ya mwili wake, na mwili wake hutikikisika.

Tangu ujana wake

"Tangu alipokuwa mtoto mdogo." Inaweza kuwa msaada kusema kama sentensi nzima. "Amekuwa hivi tangu alipokuwa mtoto mdogo"

Uwe na huruma

"hisi huruma"au " uwe na wema"

Mark 9:23

Kama uko tayari?

Yesu anakemea wasiwasi wa mtu. Hii swali linaweza kuandikwa tofauti au kama sentensi. "Yesy akamwambia, "Kwanini unasema, "kama uko tayari"? au " Yesu alimwambia, 'Usingelikuwa umesema.

unaweza

Inaweza kuwa msaada kuongeza maelezo yaliyokosekana. "unaweza kufanya lolote"

Kila kitu kinawezekana kwa yeyote aaminiye.

Hii inaweza kuandikwa kama dhahania dogo na katika kauli tendaji. "Mungu anaweza kufanya chochote kwa ajili ya watu wanaomwamini yeye"

kwa yeyote

"kwa yeyote mtu"

amini

Hii inarejea kwa kumwamini Mungu.

Nisaidie kutokuamini kwangu

Mwanaume anamuuliza Yesu kumsaidia kushinda kutoamini na kuongezea imani yake. "Nisaidie wakati ninashindwa kuamini" au "Nisaidie kuwa imani zaidi"

kundi linakimbilia kwao

Hii inamaanisha kuwa watu zaidi walikuwa wanakimbilia kule aliko Yesu na kundi lilikuwa linakuwa kubwa.

wewe roho bubu na kiziwi

Maneno "bubu" na "kiziwi" yanaweza kufafanuliwa. "Wewe roho chafu, wewe unaye sababisha kijana kutokuwa na uwezo wa kusikia na kuongea."

Mark 9:26

Alilia kwa nguvu

"Roho mchafu alilia kwa nguvu"

Mvulana alionekana kama aliyekuwa amekufa

Mvulana alionekana kufa" au Mvulana kama amekufa."

kumhangaisha mtoto

"kumtetemesha kijana"

alimtoka

Inaweza kuwa msaada kuongeza maelezo yaliyokosekana. "alitoka nje mwa kijana"

Mtoto alionekana kama amekufa

Muonekano wa kijana unalinganishwa na mtu aliyekufa.

ndipo wengi

"ndipo watu wengi"

alimchukua kwa mkono

Hii inamaanisha kuwa Yesu alimshika mkono mvulana kwa mkono wake.

mwinue juu

"alimsaidia kumwinua juu"

Mark 9:28

faragha

Hii inamaanisha walikuwa peke yao.

mtupe nje

"mtupe roho mchafu nje." Inaweza kuwa msaada kuongeza maelezo yaliyokosekana. "mtupe roho mchafu nje mwa kijana"

Aina hii haiwezi kuondoka isipokuwa kwa maombi

Neno, "haiwezekani" na "isipokuwa" yote yako kinyume. Katika lugha nyingine ni asili zaidi kutumia maelezo mazuri. "Aina hii inawezatu kuondolewa kwa maombi."

Aina hii

Hii inaelezea roho chafu.

Mark 9:30

Sentensi unganishi

Yesu na wanafunzi wake waliiacha nyumba pale walipokuwa na Yesu baada ya kumponya kijna aliyekuwa na pepo. Anatumia muda kuwafundisha wanafunzi wake peke yao.

Kupitia

Kwenda kupitia",au"Kupitia kwa"

Walienda nje ya hapo

"Yesu na wanafunzi wake waliondoka mkoa huo"

kupitia

"alisafiri kupitia"

kwa kuwa alikuwa anafundisha wanafunzi wake

Yesu alikuwa anafundisha wanafunzi wake kwa faragha, mbali na umati.

Mwana wa Adamu

Hapa Yesu anarejea kwake mwenyewe kama Mwana wa Adamu. Hili ni jina muhimu sana kwa Yesu. "Mimi, Mwana wa Adamu,"

katika mikono ya wanaume

Hapa "mikono" ni kirai cha kuthibiti. "katika udhibiti wa wanaume"

Wakati alipouwawa, baada ya siku tatu

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "Baada ya kumuua na siku tatu kupita."

walikuwa wameogopa kumuuliza

Walikuwa wameogopa kumuuliza Yesu hii sentensi ilikuwa ina maana gani. "walikuwa wameogopa kumuuliza ilimaanisha nini"

Mark 9:33

Sentensi unganishi

Wakati ambapo wanafika Karperinaumu, Yesu anafundisha wanafunzi wake kuwa watumishi wanyenyekevu.

walikuja

"walifika." Neno "wali" urejea kwa Yesu na wanafunzi wake.

kujadili

"wanajadili wao kwa wao"

walikuwa kimya

Walikuwa kimya kwa sababu waliona aibu kumwambia Yesu walichokuwa wanajadili. "walikuwa kimya kwa sababu waliona aibu"

nani alikuwa mkubwa

Hii inaweza kuwa msaada kuongeza taarifa iliyokosekana. "nani alikuwa mkubwa kati yao"

Kama yeyote anataka kuwa wa kwanza, ni lazima awe wa mwisho na mtumishi wa wote.

Hapa neno "kwanza" na "mwisho" ni maneno yanayo pishana. Yesu anazungumza kuwa "muhumimu zaidi" kama kuwa wa "kwanza" na kuwa "usiye wa muhimu zaidi" kama kuwa wa "mwisho" Kama yeyote anataka Mungu amjali ya kuwa yeye ni wa muhimu zaidi, anapaswa kujiona yeye kuwa asiye na umuhimu zaidi kwa wote"

kwa wote...kwa wote

"kwa watu wote...kwa watu wote"

Mark 9:36

katikati yao

"miongoni mwao" Neno "mwao" urejea kwa umati

Akamchukua katika mikono yake

Hii inamaanisha kuwa alimkumbatia mtoto au kumnyanyua na kumweka katika mapaja yake.

mtoto kama huyu

"mtoto kama huyu"

kwa jina langu

Hii inamaanisha kufanya kitu fulani kwa sababu ya upendo kwa Yesu. "kwa sababu wananipenda" au "kwa ajili yangu"

aliyenituma

Hii urejea kwa Mungu aliyemtuma kwa ulimwengu. "Mungu amenituma mimi"

Mark 9:38

Yohana alimwambia

"Yohana alimwambia Yesu"

fukuza mapepo

"Kuyaondoa mbali mapepo"

kaitka jina lako

Hapa "jina" lina husishwa na mamlaka ya Yesu na nguvu

hanifuati mimi

Hii ina maana kwamba hayuko miongoni mwa makundi ya wanafunzi

Mark 9:40

asiyekuwa kinyume nasi

"asiyetupinga sisi"

yuko upande wetu

Hii inaweza kuelezwa kwa usahihi inavyomaanisha. "ni kujaribu kupata malengo yale yale ambao tunayo"

Yeyote atakayekupa kikombe cha maji ya kunywa kwa sababu uko na Kristo

Yesu anazungumza kumpa yeyote kikombe cha maji kama mfano wa mtu anavyoweza kumsaidia mwingine. Huu mfano wa kumsaidia mwingine kwa njia yoyote.

hapotezi

Hii ni sentensi iliyo hasi inasisitiza maana ya chanya. Katika baadhi ya lugha, ni halisia zaidi kutumia sentensi chanya.

Mark 9:42

Jiwela kusagia

Jiwe kubwa juu yake husagwa nafaka kupataunga

kama mkono wako utakuwa kuzuizi

Hapa "mkono" ni kirai cha kutamani kufanya kitu kiovu ambacho utakifanya kwa mkono wako.

kuingia katika maisha bila mkono

"kukosa mkono na kisha kuingia katika masiha"

kuingia katika maisha

Kufa na kisha kuanza kuishi umilele kama inavyosemwa kuingia katika maisha.

bila mkono

kukosekana kwa kiungo cha mwili kwa matokeo ya kutolewa au kuumizwa. Hapa inarejea kwa kukosekana kwa mkono.

moto usiozimika

"mahali ambapo moto usiozimika"

Mark 9:45

na kutupwa kuzimu

na Mungu kuwatupa kuzimuni"

Mark 9:47

funza wake

"funza ambao hula miili ya waliokufa."

Mark 9:49

Kwa kuwa kila mmoja atakolezwa na moto.

Hapa Yesu anazungumzia kila moja atakaswe kwa kupitia mateso. Yesu anazungumzia mateso kama moto na kuwapa mteso watu kama inavyoweza kutumika kwa chumvi kwao. Hii inaweza kusemwa pia katika kauli tendi. "Kama chumvi inavyotakasa dhabihu, Mungu atamtakasa kila mmoja kwa kuwaruhu kuteseka"

ladha yake

"ina ladha ya chumvi"

utaifanyaje iwe na ladha yake tena?

Hii inaweza kuandikwa kama sentensi. "hauwezi kuifanya ladha yake tena."

ladha yake tena

"ladha ya chumvi tena"

Muwe na chumvi miongoni mwenu wenyewe

Yesu anazungumza kufanya mambo mazuri kwa kila mmoja kama hayo mazuri ni chumvi ambayo watu wanakuwa nayo. "Fanya vizuri kwa kila mmoja, kama chumvi iongezavyo ladha kwa chakula"

Mark 10

Marko 10 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri huweka nukuu kutoka kwenye Agano la Kale kwa upande wa kulia zaidi kuliko maandishi yote. ULB inafanya hivyo kwa nukuu zilizotajwa katika 10:7-8.

Dhana maalum katika sura hii

Mafundisho ya Yesu kuhusu talaka

Mafarisayo walitaka kutafuta njia ya kumlazimisha Yesu aseme kwamba ni vizuri kuvunja sheria ya Musa, hivyo wakamwuliza kuhusu talaka. Yesu anaelezea jinsi Mungu aliyepanga ndoa kwa mwanzo, kwa kuonyesha kosa la mafundisho ya talaka ya Mafarisayo.

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Mfano

Wasemaji hutumia mifano kama picha ya vitu vinavyoonekana kwa kueleza ukweli usiyoonekana. Wakati Yesu aliposema juu ya "kikombe nitakachokunywa," alikuwa akizungumzia juu ya maumivu atakapoteswa nayo msalabani kuwa mfano wa kinywaji ya uchungu na sumu katika kikombe.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Kitendawili

Kitendawili ni taarifa ya kweli inayoonekana kuelezea kitu kisichowezekana. Yesu anatumia kitendawili wakati anasema, "Yeyote anayetaka kuwa mkuu kati yenu lazima awe mtumishi wenu" (Marko 10:43).

<< | >>

Mark 10:1

Sentensi unganishi

Baada ya Yesu na wanafunzi wake kuondoka Karpenaumu, Yesu anawakumbusha Mafarisayo, pamoja na wanafunzi wake, nini Mungu anategemea katika ndoa na talaka

Yesu aliondoka eneo hilo

Wanafunzi wa Yesu walikuwa wakisafiri pamoja naye. Walikuwa wakiondoka Kapernaumu. "Yesu na wanafunzi wake waliondoka Kapernaumu"

na eneo la mbele ya Mto Yorodani

"hii ilikuwa mbele ya Mto Yorodani" au "ilikuwa ng'ambo ya Mto Yorodani"

Aliwafundisha tena

Neno "ali" urejea kwa umati

ilivyokuwa kawaida yake kufanya

"ilikuwa kawaida yake" au "alikuwa desturi yake kufanya"

Musa aliwaamuru nini

Musa alitoa sheria kwa mababu zake, ambazo walipaswa kuzifuata. "Musa aliwaamuru nini mababu wetu katika hili"

cheti cha kuachana

Hii ilikuwa ni karatasi kusema kuwa mwanamke hakuwa tena mke wake.

Mark 10:5

Mioyo yenu migumu

Wakaidi ninyi

Mark 10:7

Sio mwili tena, bali mwili mmoja

Hili ni fumbo kuonyesha muungano wa kimwili wa karibu kama mme na mke.

Mark 10:10

Walipokuwa ndani

"Wakati ambapo Yesu na wanafunzi walikuwa"

ndani ya nyumba

Wanafunzi wake Yesu walikuwa wakizungumza naye kwa faragha. walikuwa peke yao ndani ya nyumba"

wakamwuliza tena kuhusu hili

Neno "hili" urejea kwa mazungumzo aliyokuwa nayo Yesu pamoja na Mafarisayo kuhusu talaka.

Yeyote

"kama mtu yeyote"

anafanya uzinzi dhidi yake

Hapa "yake" urejea kwa mwanamke aliyemuoa kwanza

anafanya uzinzi

Inaweza kuwa msaada kuongeza taarifa zilizosahaulika. "anafanya uzinzi dhidi yake" au "anafanya uzinzi dhidi ya mme wa kwanza"

Mark 10:13

Waruhusuni waatoto wadogo waje kwangu, na msiwazuie

Sentensi hizi mbili zina maana sawa, zimerudiwa kwa ajili ya msisitizo. Katika luga zingine ni asili zaidi kusisitiza kwa njia nyingine. AT: " Muwe na uhakika wa kuwaruhusu watoto wadogo kuja kwangu."

Msizuie

Hii ni hasi mbili. Katika baadhi ya lugha ni asili zaidi kutumia taarifa chanya. AT: "ruhusu"

Mark 10:15

yeyote

"kama yeyote"

kama mtoto mdogo

Yesu analinganisha namna gani watu wanapaswa kuupokea ufalme wa Mungu na namna watoto wanavyoweza kuupokea. "katika tabia hiyo kama mtoto angefanya"

asiyeupokea ufalme wa Mungu

"hawataweza kumpokea Mungu kama mfalme wao"

hakika hawezi kuuingia

Neno "kuui" urejea kwa ufalme wa Mungu.

Kisha akawachukua watoto mikononi mwake

"aliwakumbatia watoto"

Mark 10:17

Kwanini unaniita mwema

AT: Unapaswa kufikiria kwa umakini unacho ashiria (AU, kile ambacho unaashiria nilivyo) kwa kuniita mwema, kwa sababu Mungu pekee ndiye mwema!

Mark 10:20

Unapungukiwa kitu kimoja

"Kuna kitu kimoja unapngukiwa." Hapa Yesu anazungumza juu ya tendo la kutofanya kitu fulani" kama "kupungukiwa." "Kuna kimoja ambacho haujafanya"

unapungukiwa

hauna kitu fulani

uwape masikini

Hapa neno "u" urejea kwa vitu anavyouza na ni kifungu cha maneno kinachosimama badala ya pesa mtu anayopokea anapouza. "wape masikini pesa"

masikini

Hii urejea kwa masikini. "watu masikini"

hazina

"utajiri"

alikuwa na miliki nyingi

"alimiliki vitu vingi"

Mark 10:23

Ni rahisi kwa Ngamia kupita kwenye jicho la sindano, kuliko tajiri kuingia kwenye ufaulme wa Mungu.

Haiwezekani kwa Ngamia kuingia kwenye jicho la sindano. Ni ngumu zaidi kwa watu matajiri kuamua kumruhusu Mungu atawale maisha yao."

Jicho la sindano

"Jicho la sindano" ni shimo lililo juu ya sindano.

Mark 10:26

Ni nani atakaye okolewa?

"Hivyo hakuna atakaye okolewa."

Mark 10:29

hayupo mmoja ambaye amebaki...ambaye hatapokea

"yeyote aliye acha...atapokea."

kwa ajili yangu

"kwa faida yangu" au "kwa yangu tena"

Dunia hii

"maisha haya" au "umri huu uliopo"

Dunia ijayo

"maisha yajayo" au "umri ujao"

Mark 10:32

Mwana wa Mtu atatolewa

"watu watamtoa Mwana wa Mtu" au "watu watamwachilia Mwana wa Mtu."

Mark 10:35

tu...tu

Haya maneno urejea peke yake kwa Yakobo na Yohana

katika utukufu wako

"wakati ambapo unatukuzwa." Maneno haya "utukufu wako" urejea wakati Yesu anatukuzwa na kutawala katika ufalme wake. "wakati ambapo unaongoza katika ufalme wako"

Mark 10:38

kikombe nitakacho kinywea

Yesu anatumia maneno haya kurejea kwenye mateso ambayo yuko karibu kuyapitia.

ubatizo ambao nitabatizwa kwao

Yesu anatumia maneno haya kurejea kwenye mateso ambayo yuko karibu kuyapitia.

Mark 10:41

wale wanaokusudiwa utawala

"wale wanaofikiriwa kuwa watawala

Kutawala

"kudhibiti" "kuwa na nguvu juu ya"

zoezi

"kufanya matumizi ya"

Mark 10:43

kuwa mkubwa

"kuwa katika heshima" au "Kupongezwa"

yeyote

mtu yeyote

kwa kuwa Mwana wa Mtu hakuja kutumikiwa

"Kwa kuwa Mwana wa Mtu hakuja kwa watu ili wamtumikie"

Mark 10:46

Batimausi

jina la mtu

Timausi

Hili lilikuwa ni jina la baba yake na kipofu mwombaji.

Mark 10:49

aliamuru aitwe

"aliamuru wengine wamwite"

kuwa jasiri

"usiogope"

Mark 10:51

Kuona

"uwezo wa kuona"

Mark 11

Marko 11 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri huweka kila mstari wa mashairi kwa upande wa kulia zaidi kuliko maandiko yote ili iwe rahisi kusoma. ULB hufanya hivi kwa mashairi katika 11:9-10,17, ambayo ni maneno kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

Punda na mwana-punda

Yesu aliingia Yerusalemu juu ya mnyama. Kwa njia hii alikuwa kama mfalme aliyeingia mjini baada ya kushinda vita muhimu. Pia, katika Agano la Kale, wafalme wa Israeli walikuwa wanapanda punda. Wafalme wengine walipanda farasi. Kwa hiyo Yesu alikuwa akionyesha kwamba alikuwa mfalme wa Israeli lakini hakukuwa kama wafalme wengine.

Mathayo, Marko, Luka, na Yohana wote waliandika juu ya tukio hili. Mathayo na Marko waliandika kwamba wanafunzi walimletea Yesu punda. Yohana aliandika kwamba Yesu alipata punda. Luka aliandika kwamba walimletea mwana-punda. Mathayo tu aliandika kwamba kulikuwa punda pamoja na mwana-punda. Hakuna anayejua hakika ikiwa Yesu alipanda punda au mwana-punda. Ni bora kutafsiri kila maneno haya kama yanoyoonekana katika ULB bila kujaribu kuwafanya wote wanasema jambo sawa. (Ona: Mathayo 21:1-7 na Marko 11:1-7 na Luka 19:29-36 na Yohana 12:14-15)

<< | >>

Mark 11:1

Bethfage

ni jina la kijiji

Mark 11:4

Walikwenda

"Wanafunzi wawili walikwenda"

mwanapunda

Hii urejea kwa punda mdogo aliye na uwezo wa kubeba mtu.

Walizungumza

"Waliitikia"

kama Yesu alivyowaambia

"kama Yesu alivyowaambia kuitikia." Hii inarejea namna Yesu alivyokwisha waambia kuitikia kwa maswali ya watu kuhusu kumchukua mwanapunda.

wakawaacha waende

Hii inamaanisha kuwa waliwaruhusu kuendelea kufanya walichokuwa wakifanya"

Mark 11:7

Hosana

Maana ya neno hili haiko wazi, bali kwa uhakika lilitafsiriwa vizuri zaidi kama kuelezea ukaribisho na kusifu, kama ndani "Chini" au"Kumsifu Mungu"

Mark 11:11

wakati ulikuwa umeenda

"kwa sababu ilikuwa jioni"

alikwenda Bethania pamoja nao kumi na wawili

"yeye na wanafunzi wake walikwenda Yerusalemu na kwenda Bethania"

walipokuwa wakirudi kutoka Bethania

"wakati walipokuwa wakirudi Yerusalemu kutoka Bethania"

Mark 11:13

Sentensi unganishi

Hii ilitokea wakatik Yesu na wanafunzi wake wanatembea kuelekea Yerusalemu.

kama angeweza kupata chochote juu yake

"kama kulikuwa na tunda lolote juu yake"

hakupata chochote isipokuwa majani

Hii inamaanisha kuwa hakupata mtini wowote. "alipata majani peke yake na hakuna mtini katika mti"

majira

"wakati wa mwaka"

Aliuambia, "Hakuna yeyote atakayekula tunda kutoka kwako tena

Yesu anauambie kwa mtini na kuulaani. Anazungumza nao ili wanafunzi wake wasikie.

Anauambia mti

"Alizungumza na mtu"

Na wanafunzi wake wakasikia

Neno "wa" urejea kwa Yesu anazungumza kwa mtini.

Mark 11:15

Walikuja

"Yesu na wanafunzi wake walikuja"

kuanza kuwatoa nje wauzaji na wanunuzi ndani ya hekalu

Yesu anawafukuza watu hawa nje ya hekalu. Hii inaweza kuandikwa kwa usahihi. "kuanza kuwatoa wauzaji na wanunuzi nje ya hekalu"

wauzaji na wanunuzi

"watu waliokuwa wakinunua na kuuza"

Mark 11:17

Je haikuandikwa, 'Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote'?

"Imeandikwa ndani ya maandiko kwamba Mungu alisema, 'Ninataka nyumba yangu kuitwa nyumba mahali watu kutoka mataifa yote wanapaswa kusali', lakini ninyi majambazi mmeifanya kama pango mahali mnakoweza kujificha! Ninyi mnajua hivyo!"

Mark 11:20

Mti wa mtini ulikauka mpaka kwenye mizizi yake

"mti wa mtini ulikauka mpaka kwenye mizizi yake na ulikufa."

Mark 11:22

kama hatakuwa na mashaka moyoni mwake lakini huamini

"kutokuwa na mashaka" ina maana mbili hasi "hakika amini." Vifungu hivi vyote vina maana sawa iliyorudiwa kwa mkazo. Lugha zingine zimesisitiza kwa njia tofauti. Wakati: Kama hakika huamini"

Mark 11:24

Wakati mnaposimama na kusali

Ni kawaida kwa desturi za kiyahudi kusimama wakati tusalipo kwa Mungu.

Mark 11:27

Kwa mamlaka gani mnafanya mambo haya

Maneno "mambo haya" yanalejea kwa Yesu kupindua meza za wauzaji hekaluni na kuzungumza dhidi ya vitu walivyofanya na walichofundisha.

Kwa mamlaka gani mnafanya mambo haya, na ni nani aliyewapa ninyi mamlaka ya kuyafanya.

"Hamna mamlaka kufanya mamba haya kwa sababu hatujawapa ninyi mamlaka."

Mark 11:29

Ubatizo wa Yohana, ulitoka mbinguni au ulitoka kwa watu?

Pamoja na kwamba Yesu alilijua jibu la swali hili, aliwauliza kuwajaribu viongozi wa dini sababu ya kumuuliza yeye.

Mark 11:31

Kama tukisema, 'Kutoka mbinguni'

Inaweza kuwa msaada kuongoza taarifa zilizokosekana. "Kama tukisema 'ilitoka mbinguni"

Kutoka mbinguni

Hapa "mbinguni" urejea kwa Mungu. "Kutoka kwa Mungu"

hamkumwamini

Neno "ham" urejea kwa Yohana mbatizaji.

Lakini kama tukisema 'Kutoka kwa wanadamu,'

Inaweza kuwa msaada kuongeza taarifa zinazokosekana katika majibu yao. "Lakini kama tukisema, 'kutoka kwa wanadamu"

Kutoka kwa wanadamu

"Kutoka kwa watu"

Kama tukisema, 'Kutoka kwa wanadamu;...

Viongozi wa dini hawasemi kuwa tatizo lingeweza kuwa kama wangetoa jibu hilo, lakini walifikiri juu yake. "Lakini kama tukisema, 'Kutoka kwa wanadamu, hiyo haitakuwa vizuri" au "Lakini hatutaki kusema kutoka kwa wanadamu"

Waliwaogopa watu

Mwandishi, Mariko, anaeleza kwanini viongozi wa dini hawakutaka kusema kuwa ubatizo wa Yohana ulitoka kwa wanadamu. Hii inaweza kusemwa kwa usahihi. "Walisema wao kwa wao kwa sababu waliwaogopa watu" au "Hawakutaka kusema kuwa ubatizo wa Yohana ulitoka kwa wanadamu kwa sababu waliwaogopa watu.

wote walishika

"watu waliamini"

Hatujui

Hii inaweza kuwa msaada kuongoza taarifa zinazokosekana. "Hatujui ubatizo wa Yohana ilitoka wapi"

Mark 12

Marko 12 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri huweka kila mstari wa mashairi kwa upande wa kulia zaidi kuliko maandiko yote ili iwe rahisi kusoma. ULB inafanya hivyo kwa mashairi katika 12:10-11,36, ambayo ni maneno kutoka Agano la Kale.

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Hali ya Kudhania

Hali za kudhania ni hali ambazo hazikutendeka. Watu huelezea hali hizi ili waweze kujifunza kile wasikilizaji wao wanafikiri ni nzuri na mbaya au sahihi na zisizo sahihi. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-hypo)

<< | >>

Mark 12:1

pangisha shamba la mizabibu

Mwenye shamba aliwapangisha wengine kuitunza mizabibu.

Mark 12:4

Akamtuma kwao

"mumiliki wa shamba la mzabibu alituma waoteshaji wa mzabibu"

wakamjeruhi kichwani

Hii inaweza kuandikwa kwa usahihi. "walimpiga huyo moja kwenye kichwa, na kumuumiza vibaya"

bado mwingine...wengine wengi

Haya maneno urejea kwa watumishi wengine. "bado mtumishi mwingine...watumishi wengine wengi"

Waliwatendea wengine wengi mambo kama hayo hayo.

Hii inarejea kwa watumishi waliotumwa na mwenye shamba. Maneno "hayo hayo" urejea kwa jinsi walivyotendewa. Hii inaweza kuandikwa kwa usahihi. "Waliwatendea watumishi wengine wengi waliotumwa na mwenye shamba"

Mark 12:6

Watumishi ya shamba

Wakulima wa mizabibi waliokuwa wamapangishwa shamba la mizabibu kutoka kwa mwenye shamba.

Mark 12:8

Kwahiyo, Je! Atafanya nini mmiliki wa shamba la mizabibu?

"Hivyo nitawaambia kile mwenye shamba la mizabibu atakavyofanya."

Mark 12:10

Hamjapata kusoma andiko hili?

"Sasa fikiri kwa uangalifu kuhusu haya maneno, ambayo umeshayasoma katika maandiko."

Mark 12:13

Kwanini mnanijaribu

"Ninajua mnachojaribu cha kunifanya niseme jambo lililo kinyume ili mpate nafasi ya kunishitaki."

dinari

Ni sarafu iliyokuwa na thamani ya mshahara wa siku.

Mark 12:16

Walimletea moja

"Mafarisayo na Maherodia walimletea sarafu ya serikali ya Kirumi"

Mpeni Kaisari kwa vitu vya kaisari

"Toeni kwa serikali ya Roma vitu ambavyo vinamilikiwa na serikali ya Roma

Mark 12:18

Musa alituandikia kuwa, ikiwa ndugu ya mtu...kuwa na mtoto kwa ajili ya ndugu yake.

Musa aliandika kuwa kama ndugu wa mttu akifa... ndugu yake ajipatie mtoto kwa mke aliyeachwa kwa ajili ya ndugu yake.

Mark 12:20

Wakati wa ufufuo, watakapofufuka tena, atakuwa mke wa nani?

"Katika ufufuo, watakapofufuka tena, haitawezekana tena kuwa mke wa hao ndugu saba!"

Mark 12:24

Je! Hii siyo sababu kuwa mmopotoshwa...nguvu za Mungu?

"Mmekoseshwa kwasababu hamjui maandiko wala nguvu za Mungu."

Mark 12:26

wanafufuliwa

"Mungu anawafufua"

Mark 12:28

Sentensi unganishi

Mwandishi anamuuliza Yesu swali la akili, ambalo Yesu analijibu.

Alimuuliza

"Mwandishi alimuuliza Yesu"

iliyo ya muhimu zaidi katika zote..iliyo ya muhimu ni hii

Taarifa inayokosekana inaweza kuongozwa. "amri iliyo ya muhimu zaidi katika zote...amri iliyo ya muhimu anasema"

Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu, Bwana ni mmoja.

"Sikiliza, Israeli! Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja"

kwa moyo wako yote, kwa roho yako yote

"Moyo" na "roho" ni mifano ya utu wa ndani na tamaa zake na hisia. "kwa chote unachotaka na kujisikia"

kwa akili yako yote, na kwa nguvu zako zote

"akili" urejea kwa namna mtu anavyofikiri na "nguvu" urejea kwa nguvu za mtu kufanya mambo. "kwa yote unayofikiri, na kwa yote unayofanya"

umpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe

Yesu anatumia mfanano kulinganisha namna watu wanavyopaswa kupendana wao kwa wao kwa upendo ule ule kama wanavyojipenda wenyewe"

zaidi ya hizi

Hapa neno "hizi" urejea kwa amri mbili ambazo Yesu alikuwa amewambia watu.

Mark 12:32

Sentensi unganishi

Yesu anamsifu mwandishi juu ya mawazo yake juu ya kila alichosema Yesu.

Vema

"Jibu zuri"

Mungu ni mmoja

Hii inamaanisha kuwa kuna Mungu mmoja tu.

hakuna mwingine

Iliyokosekana inaweza kuongezewa. "hakuna Mungu mwingine"

kwa moyo wote...kwa ufahamu wote... kwa nguvu zote

"Moyo" ni mfano utu wa ndani wa mtu na tamaa zake na hisia. "Ufahamu" urejea kwa kufikri na "nguvu" urejea kwa nguvu za mtu kufanya.

ule moyo...ule ufahamu...zile nguvu

Neno "ule" limewekwa katika maumbo yai ambapo neno "ako" limeachwa. Linaweza kuongezwa.

kumpenda jirani kama mwenyewe

Mfanano huu unalinganishwa namna watu wanavyopaswa kupendana wao kwa wao kwa upendo ule ule wanavyojipenda wenyewe.

ni muhimu mno kuliko

Lugha hii inamaanisha kuwa kitu fulani ni muhimu mno kuliko kitu kingine. Kwa hali hii, amri hizi mbili ni zaidi ya kumfurahisha Mungu kwamba matoleo ya kuteketeza na dhabihu.

Wewe hauko mbali na ufalme wa Mungu

Hii inaweza kusemwa katika mtindo wa chanya. Hapa Yesu anazungumza juu ya mtu aliye tayari kujitoa kwa Mungu kama mfalme kama aliye karibu kimwili kwa ufalme wa Mungu, kama inavyofananishwa na eneo halisi.

hakuna hata mmoja aliye thubutu

Hii inaweza kusemwa katika mtindo wa chanya. "kila moja aliogopa"

Mark 12:35

Je! Ni kwa jinsi gani waandishi husema Kristo ni mwana wa Daudi?

"Hawa watu hufundisha sheria ya kiyahudi lazima hawako sahihi wanaposema kwamba Kristo ni mtu tu wa kawaida wa uzao wa Mfalme Daudi!"

mwana wa Daudi

Neno "mwana" limetumika hapa kuelezea ukoo.

Ni kwa jinsi gani mwana wa Daudi?

"hivyo hawezi kuwa mwana wa Daudi!"

Mark 12:38

salamu walizopokea kwenye masoko

Nomino "salamu" inaweza kuelezwa pamoja na kitendo "salimu". Hizi salamu zilionyesha kuwa watu waliwaheshimu waandishi. "na kusalimiwa kwa heshima kwenye masoko" au "na kwa watu kuwasalimu kwa heshima kwenye masoko"

Wanakula nyumba za wajane

Hapa Yesu anawaeleza wandishi wakiwadanganya wajane na kuiba nyumba zao kama kula nyumba zao.

Hawa watu watapokea hukumu iliyo kuu

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "Mungu hakika atawahukumu kwa hukumu kuu" au "Mungu kwa hakika atawahukumu kwa ukali"

watapokea hukumu kuu kuliko

Neno "kuliko" humaanisha kulinganisha. Hapa kulinganisha ni watu wengine waliohukumiwa. "watapokea hukumu kuu kuliko watu wengine"

Mark 12:41

sarafu ndogo mbili

"sarafu mbili ndogo", ni sarafu yenye thamani kidogo

Mark 12:43

Amini nawaambia

Ni hakika ya kile ninachowaambia

sanduku la sadaka

sanduku hili lilikuwa na kukusanyia sadaka za watu wote hekaluni

vingi

vingi zaidi

umasikini

"upungufu" au "Kutokuwa na chochote"

Mark 13

Marko 13 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri huweka kila mstari wa mashairi upande wa kulia zaidi kuliko maandiko yote ili iwe rahisi kusoma. ULB inafanya hivyo kwa mashairi katika 13:24-25, ambayo ni maneno kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

Kurudi kwa Kristo

Yesu alisema mengi juu ya kile kitatokea kabla ya kurudi kwake (Marko 13:6-37). Aliwaambia wafuasi wake kwamba mambo mabaya yatatokea ulimwenguni na mambo mabaya yatawatokea kabla ya kurudi, lakini walistahili kuwa tayari kwa kurudi kwake wakati wowote.

<< | >>

Mark 13:1

Maelezo ya ujumla

Walipoondoka eneo la hekaluni, Yesu anawambia wanafunzi wake nini kitatokea badae katika hekalu zuri ambalo Herode mkuu alilijenga.

mawe haya yakushangaza na majengo

"Mawe" urejea kwa mawe yaliyotumiwa kujenge. ""majengo yakushangaza na mawe yalitokana nayo"

Unaona majengo haya makubwa? Hakuna hata jiwe moja

Hili swali linatumiwa kuleta umakini kwa majengo. Hii inaweza kuandikwa kama sentensi. "Tazama haya majengo makubwa sasa, lakini hakuna jiwe hata moja"

Hakuna hata jiwe moja litakalo salia juu ya jingine ambalo halitaangishwa chini.

Hii inamaanisha kuwa maadui wa kijeshi wataangusha mawe. Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "Hakuna jiwe hata moja litakalo salia juu ya jingine, kwa kuwa maadui wa kijeshi watakuja na kubomoa majengo haya."

Mark 13:3

Sentensi unganishi

Katika kujibu maswali ya wanafunzi kuhusu kubomolewa kwa hekalu na nini kitatokea, Yesu anawambia nini kitatokea badae.

Naye alipokuwa amekaa juu ya Mlima wa Mizeituni nyuma ya hekalu, Petro

Walipokuwa wamefika kwenye Mlima wa Mizeituni, na Yesu kuwa amekiti chini. Taarifa zinaweza kufanya kwa usahihi. "Baada ya kufika kwenye Mlima Mizeituni, ambao ulikuwa nyuma ya hekalu, Yesu chini.

faraga

"wakati ambapo walikuwa peke yao"

haya mambo yanatokea...yako karibu kutokea

Hii inarejea kwa kile Yesu amekwisha sema kitatokea kwa mawe ya hekalu. Hii inaweza kufanywa wazi. "haya mambo hutokea kwa majengo ya hekalu... yako karibu kutokea kwa majengo ya hekalu"

wakati ambapo haya yote

"kwamba haya yote"

Mark 13:5

kwao

"kwa wanafunzi wake"

kuwapotosha

Yesu anawaonya wanafunzi wake wasidaganywe na yeyote nini kitatokea. Hapa"kuwapotosha" ni mfano wa kudanganya.

kwa jina langu

Maana talajiwa ni 1)kudai mamlaka yangu" au 2) kudai kuwa Mungu amewatuma"

Mimi ndiye

"Mimi ni Kristo"

watawapotosha wengi

Hapa "kuwapotosha" ni mfano ukimaanisha kudanganya. "nitawadanganya watu wengi"

Mark 13:7

Mtakaposikia vita na tetesi za vita

Maana talajiwa ni 1)"sikia sauti halisi ya vita ikiwa karibu na taarifa za vita kwa mbali" au 2)sikia vita ambavyo ni halisia vinatokea na watu kusema kuwa vita vinaenda kuana"

tetesi

maneno ambayo siyo rahisi kugundua kama yako sahihi au hapana

lakini mwisho bado

Hii inarejea kwa mwisho wa ulimwengu. Taarifa zinazokosekana zinaweza kuongezewa. "lakini siyo mwisho wa ulimwengu. "

litainuka kinyume

Lugha hii inamaanisha kupigana na mtu mwingine. "nitapigana kinyume"

Taifa litainuka kinyume na taifa jingine

Taarifa zinazokosekana zinaweza kuongezwa. "taifa litainuka kinyume na taifa" au "taifa litapigana kinyume na taifa"

Huu ni mwanzo wa utungu.

Yesu anazungumza juu ya maafa kama mwanzo wa utungu kwa sababu mambo makali yatatokea baada ya hayo. "Haya matokeo yatakuwa kama utungu wa kwanza wa mwanamke anaposumbuka wakati anapozaa mtoto. Watasumbuka zaidi baada ya hayo"

Mark 13:9

Iweni macho

"Iweni tayari kwa yale watu watawafanyia"

watawapeleka hadi

Hii inamaanisha kuwafunga watu fulani na kuwaweka chini ya usimamizi wa mtu mwingine.

mtapigwa

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "watu watawapiga"

Mtasimamishwa mbele

Hii inamaanisha kuwekwa katika kujaribiwa na kuhukumiwa. "Mtawekwa katika kujaribiwa kabla" au "Mtaletwa katika kujaribiwa na kuhukumiwa"

kwa ajli yangu

"Kwa sababu yangu" au "kusababishwa na mimi"

kama ushuhuda kwao

Hii inamaanisha watashuhudia kuhusu Yesu. Hii inaweza kufanywa wazi. "na kuwashuhudia kuhusu mimi" au "na mtawambia kuhusu mimi"

Lakini injili lazima kwanza ihubiriwe kwa mataifa yote.

Yesu bado anazungumza juu ya mambo ambayo lazima yatatokea kabla ya mwisho kuja. Hii inaweza kufanywa wazi. "Lakini injili ihubiriwe kwanza kwa mataifa yote kabla mwish haujaja"

Mark 13:11

kuwakabidhi

Hii inamaanisha kuwaweka chini ya usimamizi wa mtu mwingine. Kwa jambo hili, chini ya uzimamizi wa mamlaka.

lakini Roho Mtakatifu

Taarifa zinazokosekana zinaweza kuongezewa. "lakini Roho Mtakatifu atazungumza kupitia wewe"

Ndugu atamshitaki ndugu kuuawa

Ndugu atamshitaki ndugu kuuawa "Ndugu atamshitaki ndugu yake kuuawa" Hii inamaanisha kuwa ndugu atamsaliti ndugu yake na kusaliti huku kutasababisha ndugu yake kuuawa

Ndugu...ndugu

Hii inarejea kwa wote ndugu na dada

baba na mtoto

Hii inamaanisha kuwa baba atamsaliti mtoto wake na kusaliti huku kutasababisha mtoto kuuawa. "baba atamshitaki mtoto wake "auwawe" au baba atamsaliti mtoto wake, kumwaacha auwawe"

Watoto watasimama kinyume cha baba zao

Hii inamaanisha kuwa watoto watawapinga wazazi wao na kuwasaliti.

kuwasababisha kuuawa

Hii inamaanisha kuwa mamlaka yatasema wauwawe. Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji.

Mtachukiwa na kila mtu

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "Kila mmoja atawachukia"

kwa sababu ya jina langu

Yesu anatumia kirai "jina langu" kurejea kwake mwenyewe. "kwa sababu yangu" au "kwa sababu mnaniamini mimi"

atakayevumilia mpaka mwisho, mtu huyo ataokoka.

Hii inamaanisha kuwa mwaminifu kwa Mungu mpaka mwisho wa maisha ya mtu. Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "Mungu atamuokoa yeyote aliye mwaminifu kwake, kuvumilia majaribu, mpaka mwisho wa maisha yake"

Mark 13:14

chukizo la uharibifu

Haya maneno yanatoka kitabu cha Daniel. Wasikilizaji wake wangekuwa na uelewa wa aya na unabii uhusuo chukizo kuingia katika hekalu kulinajisi. "mambo ya aibu yanayo najisi vitu vya Mungu.

limesimama pale lisipotakiwa kusimama

Wasikilizaji wa Yesu wangekuwa wamejua kuwa hii inarejea kwa hekalu. Hii inaweza kufanywa kwa usahihi. "kusimama katika hekalu pale lisipotakiwa"

asomaye na afahamu)

Si Yesu anazungumza. Mathayo aliongeza kwa hii kupata umakini wa wasomaji, ili waweze kusikiliza onyo hili. "ikiwezekana kila mmoja asomaye awe makini kwa onyo hili"

aliyeko juu ya nyumba

Juu ya nyumba ambapo Yesu aliishi ilikuwa tambarare, na watu wangeweza kusimama juu yake.

asirudi

Hii urejea kwa kurudi nyumbani kwake. Hii inaweza kufanywa kwa usahihi. "hakuna kurudi nyumbani mwake"

kuchukua vazi lake

"kuchukua vazi lake"

Mark 13:17

wana mtoto

Hii njia ya upole kusema kwa mtu kuwa ni mwenye mimba.

Ombeni kwamba

Ombeni kwamba wakati huu" au " Ombeni kwamba mambo haya"

baridi

"majira ya baridi" au " baridi, majija ya mvua" Hii urejea kipindi cha mwaka wakati ambapo ni baridi na isiyofurahisha

hayajawahi kutokea

"kubwa zaidi kuliko haijawahi tokea." Hii inaelezea namna ilivyo kubwa na mbaya mateso makubwa.

hayajawahi kutokea

hayajawahi kutokea "na kubwa zaidi haitatokea tena"

atakapopunguza siku

Inaweza kuwa msaada kuweka wazi "siku" zipi zinaongelewa. "atapunguza siku za mateso" au "atapunguza wakati wa mateso"

atapunguza

Hili neno halimaanishi kuwa siku zitakuwa chini ya masaa 24 kila moja, lakini zitakuwa siku chache za mateso.

hakuna mwili utakaookoka

Neno "mwili" urejea kwa watu. Hapa "kuokoka" urejea kwa wakovu wa kimwili. "hakuna yeyote atakayeokoka" Pia, maneno haya yanaweza kusemwa katika mtindo chanya. "kila mmoja atakufa"

kwa ajili ya

ustawi wa

wateule, ambao aliwachagua

kikundi cha maneno "wale aliowachagua" humaanisha kitu kile kile kama "wateule" Kwa pamoja, wanasisitiza kuwa Mungu aliwachagua watu hawa.

Mark 13:21

Maelezo ya ujumla

Biblia ya UDB hutumia mstari kama daraja kuunganisha mistari ya 21 na 22, kusema maelezo anayowambia watu ili kwamba iwe rahisi kuelewa.

Wakristo wa uongo

"watu wanaodai kuwa wao ni Kristo"

ili kwamba wa kuwadanganya

Neno linalokosekana linaweza kuongezwa. "ili kwamba kuwadanganya watu"

kama inawezekana, hata wateule

Maelezo yanayokosekana yanaweza kuongezwa. "Kama inawezekana, hata wanaweza kuwadanganya wateule" au "hata wataweza kujaribu kuwadanganya watu ambao Mungu amekwisha wachagua."

Iweni macho

"Iweni macho"

Nimwekwisha wambia haya yote kabla ya wakati

Yesu aliwambia mambo haya kuwaonya. "Nimewambia nyinyi haya yote kabla ya wakati kuwaonya"

Mark 13:24

jua litatiwa giza

Hii inaweza kuwa kati hali tendaji. "jua litatiwa giza"

mwezi hautatoa mwanga wake

Hapa mwezi umeongelewa kama ulikuwa hai na waweza kutoa kitu chochote kwa mtu fulani. "mwezi hautato mwanga" au "mwezi utatiwa giza"

nyota zitaangika kutoka angani

Hii haimanishi kwamba zitaanguka chini lakini ni kwamba zitaanguka kutoka pale zilipo kwa sasa.

nguvu zilizoko mbinguni zitatikisika

Hii inaweza kuwa kati hali tendaji. "Mungu ataitingisha nguvu zilizoko mbinguni"

nguvu

Hili ni jina la maelezo juuya sayari na linaweza kuwa pamoja na nyote.

mawinguni

"mawinguni"

Kisha watamuona

"Kisha watu watamuona"

kwa nguvu kubwa na utukufu

"nguvu na utukufu"

atawakusanya

Neno "ata" urejea kwa Mungu na kirai kwa malaika wake, kama wao watakao kusanya wateule. "watawakusanya" au "malaika wake watawakusanya"

pande kuu nne

Ulimwengu wote umesemwa kuwa kama "pande kuu nne" ambazo zinarejea kwa pande nne: kaskazini, kusini, mashariki, na magharibi.

kutoka mwisho wa dunia mpaka mwisho wa mbingu.

Huku kulikokithiri kumetolewa msisitizo kwamba wateule watakusanywa kutoka ulimwengu wote. "kutoka kila eneo ulimwenguni"

Mark 13:28

Sentensi unganishi

Yesu anatoa mifano mifupi hapa kuwakumbusha watu kufahamu lini mambo aliyokuwa anaongelea yanatokea

tawi liwezavyo kutoa

Kifungu "tawi" urejea kwa matawi ya mtini. "matawi yake yanaweza kutoa"

kutoa

"ukijani na laini"

kuweka majani

Hapa majani ya mtini yanaongelewa kama yalikuwa hai na yanaweza kuwa tayari kusababisha majani yake kukua. "majani yake huanza kuchipua"

kiangazi

sehemu ya mwaka ni joto au majira ya kukua

mambo haya

Hii inarejea kwa siku za mateso. "mambo haya nimekwisha kueleza"

yuko karibu

"Mwana wa Adamu yuko karibu"

karibu na malango

Nahau hii inamaanisha kwamba yuko kairba na karibu ameshafika, urejea kwa msafiri kuwa karibu kufika katika mlango. "na yuko karibu hapo"

Mark 13:30

Kweli, nawambieni

Hii huonyesha kwamba sentensi inayofuata hasa ni kweli na muhimu.

hakitapita

Ni njia ya kistaarabu kusema juu ya mtu fulani kufa. "hatakufa" au "hatakoma"

mambo haya hayajatokea

Kifungu "mambo haya" urejea kwa siku za mateso.

Mbingu na nchi

Huku kulikokithiri kunarejea mbingu zote, pamoja na jua, mwezi, nyote, na sayari na ulimwengu wote.

zitapita

"itakoma kuishi" Kifungu hiki urejea kwa mwisho wa ulimwengu.

maneno yangu hayatapita kamwe

Yesu huzungumza maneno yakutopoteza nguvu zao kama wangekuwa kitu fulani ambacho kamwe hakitakufa. "maneno yangu kwamwe hayatawapotezea nguvu zao"

siku hiyo au saa hiyo

HIi urejea kwa wakati ambapo Mwana wa Adamu atarudi. "siku hiyo au saa hiyo ambapo Mwana wa Adamu atarudi" au " siku hiyo au saa hiyo ambapo nitarudi"

hata malaika wa mbinguni, wala Mwana

Haya yametajwa kati ya wale wasiojua lini Mwana wa Adamu atarudi. "hata malaika mbinguni au Mwana anajua"

malaika mbinguni

Hapa "mbinguni" urejea kwenye eneo ambalo Mungu huishi.

ila Baba

Ni vizuri kutofasiri "Baba" na neno hilo ambalo lugha yako ya asili hutumia kurejea kwa baba wa kibinadamu. Pia, hii ni umboyai ambayo husema kwamba Baba anajua lini Mwana atarudi. "ila ni Baba anajua"

Mark 13:33

muda gani yatatokea

Inaweza kuanishwa waziwazi nini "muda" urejea kwa. "wakati ambapo muda utakuja wakati ambapo matukio yote haya yatatokea"

kila mmoja na kazi yake

"kuwaambia kila moja kazi gani anapaswa kufanya"

Mark 13:35

kama ni jioni

Hii urejea kwa kurudi kwa bwana. "kama atarudi jioni"

jogoo atakapowika

Jogoo ni ndege anayeita asubuhi na mapema. Sauti kubwa anayofanya ni "kuwika"

asikukute umelala

Hapa Yesu anazungumza kutokuwa tayari kama "kulala" "asikukute hauko tayari kwa kurudi kwake"

Mark 14

Marko 14 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri huweka kila mstari wa mashairi kwa upande wa kulia zaidi kuliko maandiko yote ili iwe rahisi kusoma. ULB inafanya hivyo kwa mashairi katika 14:27,62, ambayo ni maneno kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

Kula mwili na damu

Marko 14:22-25 inaelezea chakula cha mwisho cha Yesu na wafuasi wake. Wakati huu, Yesu aliwaambia kwamba kile walichokuwa wakila na kunywa kilikuwa mwili wake na damu yake. Karibu makanisa yote ya kikristo huadhimisha "Meza ya Bwana," "Ekaristi", au "Mkutano wa Kikawa" kukumbuka chakula hiki.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Abba, Baba

"Abba" ni neno la Kiaramu ambalo Wayahudi walitumia kuzungumza na baba zao. Marko analiandika kama linavyotamkwa na kisha kulifasiri. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-transliterate)

"Mwana wa Mwanadamu"

Yesu anajiita mwenyewe "Mwana wa Binadamu" katika sura hii (Marko 14:20). Lugha yako huenda haiwezi kuwaruhusu watu kujizungumzia wenyewe kana kwamba wanaongea juu ya mtu mwingine. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sonofman and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-123person)

<< | >>

Mark 14:1

Sentensi unganishi

Siku mbili tu kabla ya pasaka, makuhani wakuu na waandishi walikuwa wakitafuta kwa hila namba ya kumuua Yesu.

hila

pasipo watu kugundua

Kwa kuwa walisema

Neno "wa" urejea kwa makuhani wakuu na waandishi.

Sio wakati huu wa sikukuu

Inaweza kuwa msaada kuongoze taarifa zilizokosekana. "Hatuwezi kufanya wakati wa sikukuu"

Mark 14:3

Simoni Mkoma

Huyu mtu alikuwa na ukoma hapo awali lakini hakuwa mgonjwa tena.

alabaster

Hili ni laini, "jiwe jeupe."

Nini sababu ya upotevu huu?

Hakuna sababu nzuri kupoteza manukato ghali namna ile.

Manukato haya yangeweza kuuzwa

"Tungeuza manukato haya." au Angeweza kuuza manukato haya

dinari mia tatu

"dinari 300." Dinari ni sarafu za Kirumi.

Mark 14:6

Kwa nini mnampa shida?

Hampaswi kumpa shida

Mark 14:10

Sentensi unganishi

Baada ya mwanamke kumpaka mafuta Yesu kwa manukato, Yuda anaahidi kumkabidhi kwa mahuni wakuu.

ili kwamba apate kumkabidhi kwao

Yuda hakumkabidhi Yesu kwao bado, badala yake alienda kufanya mipango nao. "ili kufanya mpango nao kumkabidhi Yesu kwao"

Wakati wakuu wa Makuhani waliposikia hivyo

Inaweza kuwa msaada kusema waziwazi nini makuhani wakuu walisikia. "Wakati ambapo makuhani wakuu walisikia nini alichotaka kufanya kwa ajili yao"

Mark 14:12

chumba cha wageni

chumba cha ziada kwa ajili ya watembeleaji

Mark 14:15

Fanyeni maandalizi kwa ajili yetu pale

Walipaswa kufanya maandalizi ya chakula cha Yesu na wanafunzi wake kula. "Andaa chakula kwa ajili yetu hapo"

wanafunzi waliondoka

"Wanafunzi wawili waliondoka"

alivyokuwa amewaambia

"kama Yesu alivyokuwa amesema"

Mark 14:17

Karibia meza

Ilikuwa desturi kuwa na meza fupi ikiwa na mito ambapo wageni wangeweza kukaa mbele katika mkao wa nusu kulala kwenye meza wakati wa karamu ya chakula.

mmoja baada ya mwingine

Hii ina maana kwamba "mmoja kwa muda wake" kila mwanafunzi alimwuliza yeye.

Hakika si mimi?

"Hakika, haiwezi kuwa mimi ninayesaidia adui zako kukukamata!"

Mark 14:20

Ni moja wa kumi na wawili kati yetu

"Yeye ni mmoja wa kumi na wawili, mmoja kwa sasa"

anachovya tonge katika bakuli pamoja nami.

Katika utamaduni wa Yesu, wate wangeweza kula mara chache mkate, kuchovyo katika bakuli la mchuzi.

Kwa kuwa Mwana wa Adamu atakwenda kama vile maandiko yasemavyo juu yake

Hapa Yesu urejea kwa maandiko kutabiri kuhusu kifo chake. Kama una njia ya kistaraabu kusema kuhusu kifo katika kabila lako, tumia hapa. "Kwa kuwa Mwana wa Adamu atakufa kama yasemavyo maandiko"

kupitia yeye Mwana wa Adamu atasalitiwa

Hii inaweza kuanishwa zaidi moja kwa moja. "nani anamsaliti Mwana wa Adamu"

Mark 14:22

mkate

Huu ulikuwa ni mkate ulio bapa ambao haujatiwa chachu, ambao uliliwa kama sehemu ya chakula cha pasaka

kuumega

Hii inamaanisha kwamba aliumega katika vipande ili kwamba watu wale.

Alichukua kikombe

Hapa "kikombe" ni kirai cha mvinyo. "Alichukua kikombe cha mvinyo"

Hii ni damu yangu ya agano, damu imwagikayo kwa ajili ya wengi

Agano ni kwa ajili ya msamaha wa dhambi. Hii inaweza kuandikwa kwa uwazi zaidi. "Hii ni damu yangu ambayo inathibitisha agano, damu imwagikayo ili kwamba wengi wapokee msamaha wa dhambi"

Hii ni damu yangu

"Mvinyo huu ni damu yangu. Ni vizuri kutofasiri kihalisia, ijapokuwa wengi huelewa hii kumaanisha kwamba mvinyo unawakilisha damu ya Yesu na huo mvinyo si damu halisi.

Kweli nawaambia

Hii inaonyesha kuwa sentensi inayofuata hasa ni kweli na muhimu.

zao hili la mzabibu

"mvinyo" Hii ni njia ya maelezo inayorejea kwa mvinyo.

mpya

Maana zinazowekana ni 1) "tena" au 2)"kwa njia mpya"

Mark 14:26

wimbo

Wimbo ni aina ya wimbo. Ilikuwa desturi yao kuimba Zaburi toka Agano la Kale katika haua hii.

Mark 14:28

Hata kama wote watajitenga, mimi sitaku

"Sitaku" ni kifupi cha sitajitenga nawe. Maneno "jitenga nawe" yanarudia kinyume chake mara mbili na humaanisha "nitabaki na wewe."

Mark 14:30

kunikana

"sema kwamba hunijui mimi"

Mark 14:32

roho

Neno "roho" limetumika wakati mwingine kimfano kurejea kwa mtu kamili siyo sehemu yake tu.

Mark 14:35

saa hii ingempita

"apewe nguvu ya kushinda mateso aliyokuwa anayapitia.

Aba

Abba ni neno la Kiyunanai ambalo linatumika na watoto kumtaja baba yao. Inaashiria uhusiano wa karibu. Kwa kuwa tayari inamtaja Baba, ni muhimu kuhifadhi neno la Kiyunani "Abba."

Niondolee kikombe hiki

Kikombe hurejea kwenye ghadhabu ya Mungu ambayo ilikuwa lazima Yesu aivumilie.

Alisema, Aba,... Baba, .... Niondolee kikombe hiki. Lakini siyo kwa matakwa yangu, bali matakwa yako."

Yesu alimwomba Baba yake kuondoa mateso ambayo angeweza kuyavumilia juu ya msalaba kufa kwa ajili ya dhambi zote za mwanadamu, kwa muda wote. Lakini Baba alihitaji dhabihu ya Mwana wake, mkamilifu wa pekee kukidhi utakatifu wake wa Kimungu. Kwa hiyo, Yesu alikwenda msalabani.

Baba

Hii ni kichwa muhimu kwa ajili ya Mungu.

Mark 14:37

akawakuta wamelala

"na akamkuta Petro, Yakobo, na Yohana wamelala"

Simoni, je umelala

"Simoni, umelala wakati nilipokuambia kukesha."

Hukuweza kukesha... saa?

"Ungeweza hata kukesha."

Roho inataka kabisa, lakini mwili ni dhaifu.

"Miili yenu haiwezi kufanya kile ambacho akili zenu zinataka ninyi kufanya."

mwili

"mwili unaoonekana"

Mark 14:40

aliwakuta wamelala

"aliwakuta Petro, Yohana, na Yakobo wamelala"

Bado mmelala na kupumzika

bado mmelala! mmepumzika!

Mark 14:43

wakamkamata

wakamkamata kwa nguvu

Mark 14:47

Je mmekuja kunikamata kwa mapanga na marungu kama mimi ni mnyang'anyi?

mnakuja kwangu, kama dhidi ya mwizi, kwa mapanga na marungu kunikamata

Mark 14:51

shuka zito la kujifunika

nguo nzito iliyotengenezwa kutokana na mmea

Mark 14:53

Sentensi unganishi

Baada ya umati wa makuhani wakuu, waandishi, na wazee kumuongoza Yesu kwa kuhani mkuu, Petro anamtazama kwa mbali wakati wengine wanasimama kushuhudia uongo kinyume na Yesu.

Pale walikusanyika pamoja naye makuhani wakuu wote, wazee, waandishi.

Hii inaweza kupangiliwa kwa upya ili kwamba inakuwa rahisi zaidi kuelewa. "Makuhani wakuu wote, wazee, na waandishi walikuwa wamekusanyika hapa kwa pamoja"

Sasa

Neno hili linatumika hapa kuweka alama ya badiliko katika hadidhi kama mwandishi anavyoanza kusema kuhusiana na Petro.

kuelekea kwenye ua wa kuhani mkuu.

Kama Petro alivyomfuata Yesu, alisimama katika uwanja wa kuhani mkuu. Hii inaweza kuandikwa waziwazi. "na alienda mpaka uwanja wa kuhani mkuu"

Aliketi pamoja na walinzi

Petro aliketi pamoja na walinzi waliokuwa wakifanya kazi katika uwanja. "Aliketi katika uwanja pamoja na walinzi"

Mark 14:55

Sasa

Hili neno limetumika kuweka alama kwa badiliko katika hadithi kama mwandishi anavyoendelea kutuambia kuhusu Yesu kuwekwa kwenye majaribio.

wapate kumwua

Hapakuwa wenyewe ambao wangemwadhibu kifo Yesu; badala yake, wangemuomba mwingine kufanya . "wangemwadhibu kifo Yesu" au "wangeweza kupata mwingine kumwadhibu kifo Yesu"

Lakini hawakuupata

Hawakupata ushuhuda kinyume dhidi ya Yesu ambao wangemtia hatiani na kumwua.

walileta ushuhuda wa uongo dhidi yake

Hapa anaongea ushuhuda wa uongo unoelezwa kama ilikuwa kama kitu halisi ambacho mtu anaweza kubeba. "Mshitaki kwa kusema ushuhuda wa uongo dhidi yake"

hata ushahidi wao haukufanana

Hii inaweza kuandikwa kwa mtindo wa chanya. "lakini ushuhuda wao haukufanana"

Mark 14:57

Tulimsikia

Neno "tu" hurejea kwa watu walioeta ushahidi wa uongo dhidi ya Yesu.

Mark 14:60

alisimama katikati yao

"alisimama kati ya wakuu wa makuhani, waandishi na wazee"

Mimi nipo

Hili ndilo jina Mungu alijiita mwenyewe katika Agano la Kale.

Mark 14:63

alirarua vazi lake

ishara ya hasira juu ya kile ambacho Yesu alikuwa amesema

Wote walimhukumu

"Wajumbe wote wa Baraza walimhukumu Yesu"

Mark 14:66

Sentensi unganishi

Kama Yesu alivyokuwa ametabiri, Petro anamkana Yesu mara tatu kabla ya jogoo hajawika.

chini ya uani

"nje ya uani"

mmoja wa wasichana wa kuhani mkuu

Mtumishi wa kike alimtumikia kuhani mkuu. "moja wa watumishi wa kike waliomtumikia kuhani mkuu"

alimkana

Hii inamaanisha kudai kwamba kitu fulani si sahihi. Katika hali hii, Petor alikuwa akisema kwamba alichosema mtumishi wa kike kuhusu yeye hakikuwa sahihi.

Sijui wala sielewi kuhusu kile unachosema

Ote,"kujua" na "kuelewa" zina maana ile ile hapa. Maana imerudiwa kuongeza msisitizo kwa kile alichokuwa akisema Petor. "Hakika sikuelewi unachoongelea"

Mark 14:69

mmoja wao

mmoja wa wanafunzi wa Yesu

Mark 14:71

naye alihuzunika na kulia

Petro alihuzunika sana na kushitushwa sana na kuanza kulia

Mark 15

Marko 15 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

"Pazia la hekalu likagawanyika mara mbili"

Pazia la hekalu lilikuwa ni ishara muhimu ambalo lilionyesha kwamba watu walihitaji kuwa na mtu anayeongea na Mungu kwa niaba yao. Hawangeweza kuzungumza na Mungu moja kwa moja kwa sababu watu wote ni wenye dhambi na Mungu huchukia dhambi. Mungu akagawanya pazia ili kuonyesha kwamba watu wa Yesu wanaweza sasa kuzungumza na Mungu moja kwa moja kwa sababu Yesu amelipia dhambi zao.

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Kudhihaki

Kwa kujifanya kumwabudu Yesu (Marko 15:19) na kwa kujifanya kuzungumza na mfalme (Marko 15:18), askari na Wayahudi walionyesha kwamba walimchukia Yesu na hawakuamini kwamba alikuwa Mwana wa Mungu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-irony and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#mock)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Eloi, Eloi, lama sabakthani?

Hili ni tamko katika Kiaramu. Marko hutafsiri sauti zake kwa kuandika kwa kutumia herufi za Kigiriki. Halafu anaelezea maana yake. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-transliterate)

<< | >>

Mark 15:1

Wewe umesema hivyo

"Wewe mwenyewe umesema hivyo."

Mark 15:9

funguliwa

"Alimpeleka mbali" au "basi nenda"

Mark 15:14

Walimpiga Yesu

Walimpiga Yesu hasa kwa fimbo

yeye alimtoa

Ona jinsi ulivyotafsiri mstari huu katika

Mark 15:16

kambini

Hii ni sehemu wanaokaa maaskari.

kikosi

"Idadi kubwa" au "wengi"

Wakamvika Yesu vazi la zambarau

Hii ilikuwa tendo la kejeli. Zambarau ilikuwa rangi inayoonesha mamlaka na kumvalisha ni namna ya kudhihaki cheo chake, "Mfalme wa Wayahudi."

Wakaanza kumpigia kumdhihaki na kusema, "salaam, Mfalme wa Wayahudi!"

Maaskari walimdhihaki Yesu kwa sababu hawakuamini kwamba alikuwa Mfalme wa Wayahudi.

Mark 15:25

majambazi

"wezi kila upande"

Mark 15:36

siki mvinyo

"siki"

Pazia la hekalu liligawanyika mara mbili

Mungu aligawa pazia la hekalu mara mbili

Mark 15:39

Mwana wa Mungu

Hii ni cheo muhimu kwa Yesu.

Salome

Ni jina.

Mark 15:45

kaburi lile lililochimbwa katika mwamba

"awali lile kaburi lilichimbwa na mtu katika mwamba imara"

sanda

vazi lililotengenezwa kwa kitani inayopandwa kama ilivyotafsiriwa katika 14:51-52

mahali pale alipozikwa Yesu

"mahali pale ambapo Yusufu na wengine waliuzika mwili wa Yesu"

Mark 16

Marko 16 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Kaburi

Kaburi ambamo Yesu alizikwa (Yohana 19:41) lilikuwa ni aina ya kaburi ambalo familia za Kiyahudi za matajiri zilizika maiti yao. Kilikuwa chumba halisi kilichokatwa kutoka kwenye mwamba. Kilikuwa na eneo bapa upande mmoja ambapo wangeweza kuweka mwili baada ya kuupaka mafuta na manukato na kuufunga kwa nguo. Kisha wangeuweka mwamba mkubwa mbele ya kaburi ili yeyote asiweze kuona ndani au kuingia.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Kijana mmoja aliyevalia vazi nyeupe

Mathayo, Marko, Luka, na Yohana wote waliandika juu ya malaika waliovalia nguo nyeupe wakiwa na wanawake katika kaburi la Yesu. Waandishi wawili kati yao waliwaita wanaume, lakini ilikuwa tu ni kwa sababu tu malaika walikuwa katika hali ya kibinadamu. Waandishi wawili kati yao waliandika kuhusu malaika wawili, lakini wale waandishi wengine wawili waliandika juu ya mmoja tu. Ni bora kutafsiri kila moja ya vifungu hivi kama inavyoonekana katika ULB bila kujaribu kufanya vifungu vyote kufanana. (See: Matthew 28:1-2 and Mark 16:5 and Luke 24:4 and John 20:12)

__<< | __

Mark 16:1

Sentensi unganishi

Siku ya kwanza ya wiki, wanawake walikuja asubuhi kwa sababu walitegemea kutumia kitoweo kuupaka mafuta mwili wa Yesu. Walishangaa kumuona kijana ambaye anawambia kuwa Yesu yu hai, lakini wanaogopa na hawamwambii mtu yeyote.

Wakati sabato ilipokwisha

Hii ni kwamba, wakati jua lilipochomoza siku ya saba na siku ya kwanza ya wiki kuanza.

Mark 16:3

jiwe lilikuwa limevingirishwa

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "mtu amekwisha kulivingirisha jiwe"

Mark 16:5

Amefufuka!

Malaika kwa mkazo anatangaza kuwa Yesu amekwishafufuka. Hii inaweza kutofasiriwa katika kauli tendaji. "Alinuka!" au " Mungu alimwinua kutoka mauti!"

Mark 16:8

kaburi,sehemu ya kuzikia

Neno "kaburi" inarejea kwenye eneo ambapo watu wanaweka mwili wa mtu aliyekufa. "Sehemu ya kuzikia" ni neno la kiujumla ambalo linarejea kwa:

walishangazwa

Haya maneno urejea kwa kushangazwa kwa sababu ya kitu cha ajabu kilichofanyika.

Mark 16:9

Sentensi unganishi

Yesu anaonekana mara ya kwanza kwa Mariamu Magidalena, ambaye anawambia wanafunzi, kisha anajitokeza kwa wengine wawili kama wanavyokuwa wakitembea, na badae anatokea kwa wanafunzi kumi na mmoja.

siku ya kwanza ya juma

"jumapili"

Walisikia

"Walimsikia Mariamu Magidalena akisema"

Mark 16:12

akajitokeza katika namna tofauti

Yesu alikuwa ni mtu ambaye "wale wawili" waliona, lakini walichokiona hakikuonekana kama Yesu, kwa hiyo hawakujua walikuwa wakimtazama Yesu

wengine wawili

wawili "wale walikuwa naye"

hawakuwaamini

Wanafunzi wengine hawakuwaamini wale wawili walikuwa wakitembea walichosema.

Mark 16:14

Sentensi unganishi

Wakati ambapo Yesu anakutana na kumi na moja, anawakemea kwa kutokuwa na imani na kuwambia waende kwa ulimwengu wote kuhubiri injili.

kumi na moja

Hawa ni wanafunzi kumi na moja ambao walibaki baada ya Yuda kuwaacha.

walikuwa wameegama katika meza

Hiki ni kirai cha kula, ambacho kilikuwa ni njia ya kawaida siku zile wakati wa kula. "walikuwa wanakula chakula"

kueegama

Walikuwa wameegama chini upande wa kushoto, wakitumia mkono wao wa kula chakula kwenye meza.

mioyo migumu

Yesu anakemea wanafunzi wake kwa sababu wasingeweza kumwamini. Tofasiri usemi huu ili ieleweke kuwa wanafunzi hawakumwamini Yesu. "kukataa kuamini"

Nenda katika ulimwengu

Hapa "ulimwengu" ni kirai kwa watu katika ulimwengu. "Nenda kila sehemu kuna watu"

ulimwengu wote

Hii ni kutia chumvi na kirai kwa ajili ya watu "ulimwengu wote"

Yeye abatizae na akabatizwa ataokolewa

Neno "a" urejea kwa yeyote. Sentensi hii inaweza kufanywa katika kauli tendaji."Mungu atawaokoa watu wote ambao wanaamini na kukuruhu wewe uwabatize"

yeye asiye amini atahukumiwa

Neno "a" urejea kwa yeyote. Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. " Mungu atahukumu watu wote ambao hawaamini."

Mark 16:17

Ishara hizi zitaambatana na wote waaminio

Mariko anasema juu ya miujiza kama vile watu wanaenda pamoja na wakristo. "Watu wanawatazama wale wanaomini wataona mambo haya kutokea na kujua niko pamoja na wakristo"

Kwa jina langu

Maana zinaweza kuwa 1) Yesu anataja orodha ya kiujumla: "Katika jina langu watafanya mambo kama haya: Wa" au 2) Yesu anatoa orodha sahihi: "Haya ni mambo watakayo fanya katika jina langu"

Katika jina

Hapa "jina" linahusishwa na mamlka ya Yesu na nguvu. "Kwa nguvu ya jina langu" au " Kwa nguvu za jina langu

Mark 16:19

akachukuliwa juu mbinguni na ameketi

Hii inaweza kuwa kusemwa katika kauli tendaji. "Mungu alimchukua juu mbinguni, na ameketi"

mkono wa kuume wa Mungu

"sehemu ambapo Mungu umpe kuketi kwa heshima na nguvu"

kulithibitisha neno

"kulionyesha kuwa maneno yake, ambayo yalikuwa yakizunguzwa, yalikuwa kweli"

Utangulizi wa injili ya Luka

Sehemu ya 1: Utangulizi wa Ujumla

Maelezo ya Kitabu cha Luka

  1. Utangulizi na kusudi la kuandika (1:1-4)

  2. Kuzaliwa kwa Yesu na maandalizi ya huduma yake (1:5-4:13)

  3. Huduma ya Yesu huko Galilaya (4:14-9:50)

  4. Safari ya Yesu kwenda Yerusalemu

  5. Yesu huko Yerusalemu (19:45-21:4)

  6. Mafundisho ya Yesu kuhusu kuja kwake mara ya pili (21:5-36)

  7. Kifo cha Yesu, kuzikwa kwake na ufufuo wake (22:1-24:53)

Je, kitabu cha Luka kinahusu nini?

Injili ya Yohana ni moja ya vitabu vinne katika Agano Jipya ambavyo huelezea baadhi ya maisha ya Yesu Kristo. Waandishi wa Injili waliandika juu ya mambo mbalimbali kuonyesha kuwa Yesu alikuwa nani na ni nini alichofanya. Luka aliandika injili yake kwa mtu aitwaye Theofilo. Luka aliandika maelezo sahihi ya maisha ya Yesu ili Theofilo awe na uhakika wa ukweli. Hata hivyo, Luka alitarajia injili kuwatia moyo waumini wote, si Theofilo tu.

Je, kichwa cha kitabu hiki kinapaswa kutafsiriwaje?

Watafsiri wanaweza kuchagua kuita kitabu hiki kwa kichwa chake asilia, "Injili ya Luka" au "Injili Kulingana na Luka." Au wanaweza kuchagua kichwa cha wazi zaidi, kama vile "Habari Njema Kuhusu Yesu "kama ilivyoandikwa na Luka." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-names)

Nani aliandika Kitabu cha Luka?

Kitabu hiki hakitupatia jina la mwandishi. Aliyeandika kitabu hiki aliandika pia Kitabu cha Matendo. Katika sehemu zimoja za Kitabu cha Matendo, mwandishi hutumia neno "sisi." neno hili linaonyesha kuwa mwandishi huyu alisafiri na Paulo. Wasomi wengi wanadhani kwamba Luka alikuwa huyu mtu aliyesafiri na Paulo. Kwa hiyo, tangu nyakati za awali za Kikristo, Wakristo wengi walidhani kuwa Luka alikuwa mwandishi wa Kitabu cha Luka na Kitabu cha Matendo.

Luka alikuwa daktari. Uandishi wake unaonyesha kuwa alikuwa mtu wa elimu. Huenda alikuwa mtu wa mataifa. Labda Luka mwenyewe hakuhuhudia vile Yesu alivyosema na alivyofanya'. Lakini alisema kuwa alizungumza na watu wengi ambao walishuhudia matendo yake.

Sehemu ya 2: Dhana muhimu za Kidini na za Kitamaduni

Je, wanawake wana majukumu gani katika Injili ya Luka?

Luka aliwaelezea wanawake kwa njia nzuri sana katika injili yake. Kwa mfano, mara nyingi alionyesha wanawake kuwa waaminifu zaidi kwa Mungu kuliko wanaume wengi. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faithful)

Kwa nini Luka anaandika mengi kuhusu wiki ya mwisho ya maisha ya Yesu?

Luka aliandika mengi juu ya wiki ya mwisho wa Yesu. Alitaka wasomaji wake kufikiri sana juu ya wiki ya mwisho wa Yesu na kifo chake msalabani. Aliwataka watu kuelewa kwamba Yesu kwa hiari alikufa msalabani ili Mungu awasamehe kwa ajili ya dhambi. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

Sehemu ya 3: Masuala muhimu ya Tafsiri

Je, vitabu vya sinoptiki vya Injili ni vipi?

Vitabu vya Mathayo, Marko na Luka huitwa injili za sinoptiki kwa sababu vina vifungu vingi vinavyofanana. Neno "synoptic" linamaanisha "kuona kwa pamoja."

Maandiko husemekana kuwa "sawa" wakati ambapo injili mbili au tatu zinafanana au zinakaribia kufanana. Wakati wa kutafsiri vifungu sambamba, wafasiri wanapaswa kutumia maneno sawa na kuyafananisha iwezekanavyo.

Je, kwa nini Yesu anajiita mwenyewe kama "Mwana wa Binadamu"?

Katika Injili, Yesu anajiita mwenyewe "Mwana wa Binadamu." Ni kumbukumbu ya Danieli 7:13-14. Katika kifungu hiki kuna mtu anayeelezewa kuwa "Mwana wa binadamu." Hiyo ina maana kwamba mtu huyo alifanana na mwanadamu. Mungu alitoa mamlaka kwa mwana wa binadamu kutawala mataifa milele. Na watu wote watamwabudu milele.

Wayahudi wa wakati wa Yesu hawakutumia "Mwana wa Binadamu" kama jina la mtu yeyote. Kwa hiyo, Yesu aliitumia kwa ajili yake mwenyewe ili kuwasaidia kuelewa yeye alikuwa nani. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sonofman)

Kutafsiri jina "Mwana wa Binadamu" kunaweza kuwa vigumu kwa lugha nyingi. Wasomaji wana uwezo wa kutoelewa tafsiri halisi. Watafsiri pia wanaweza kutumia jina mbadala, kama vile "Yule aliye Mtu." Inaweza pia kusaidia wanapoingiza maelezo ya chini ili kulielezea.

Je, ni yapi masuala makuu katika maandishi ya Kitabu cha Luka?

Hizi ndizo masuala muhimu sana katika Kitabu cha Luka:

Kifungu kinachofuata hakijaingizwa katika matoleo mengi ya kisasa. Matoleo mengine yanaiweka kwenye mabano ya mraba:

(See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/jit.html#translate-textvariants)

Luke 1

Luka 01 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri hupendelea kuweka sala ndefu au unabii mbele kidogo ya maandiko nyingine. Kwa sababu hii, ULB na tafsiri nyingine nyingi za Kiingereza huingiza mistari ya 1:46-55, 68-79.

Dhana maalum katika sura hii

"Ataitwa Yohana"

Haikuwa jambo la kawaida katika ichi ya Mashariki ya Karibu kumwia mtoto jina ambalo sio jina la jamaa. Kwa kuwa Elizabeti na Zakaria hawakuwa na mtu aliyeitwa "Yohana" katika familia yao, jina hili liliwashangaza sana kwa watu wengine.

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Luka hatumii maneno mengi magumu. Lugha yake ni rahisi na ya moja kwa moja.

| >>

Luke 1:1

Taarifa kwa Ujumla

Luka anaeleza kwanini anamwandikia Theofilo.

mada

"taarifa" au "simulizi za kweli"

kati yetu

Neno "yetu" katika kauli hii linaweza au haliwezi kutomhusisha Theofilo.

Alikabidhi kwetu sisi

"Sisi" katika kauli hii Theofilo hahusiki.

Kabidhiwa kwao

"kupewa wao" au "iliyotolewa kwao"

Watumishi wa ujumbe

Unaweza kuhitaji kupambanua kwamba ujumbe ni nini. NI: "kumtumikia Mungu kwa kuwaambia watu habari zake" au "kufundisha watu habari njema kuhusu Yesu"

Ilichunguzwa kwa uangalifu

"kutafiti kwa makini." Luka alikuwa makini kutafuta uhakika wa kile kilichotokea. Huenda alizungumza na watu mbalimbali ambao waliona kilichotokea kuhakikisha anachokindika kuhusu tukio hili ni sahihi.

Mheshimiwa sana Theofilo

Luka alisema hivi kuonesha heshima na taadhima kwa Theofilo. Hii inaweza kumaanisha kwamba Theofilo alikuwa afisa mhimu serikalini. Sehemu hii tumia mfumo unaotumika kwenye utamaduni wako kumwongelea mtu mwenye mamlaka ya juu. Baadhi ya watu wanaweza kupendelea pia kuweka salamu mwanzoni na kusema "kwa ... Theofilo" au "Mpendwa ... Theofilo."

Mheshimiwa sana

"mheshimiwa" au "muungwana"

Theofilo

Jina hili linamaana "rafiki wa Mungu." Linaweza likaweka wazi tabia ya mtu huyu au inaweza kuwa ndilo jina lake halisi. Tafsiri nyingi limetumika kama jina lake.

Luke 1:5

Kauli unganishi:

Malaika anatoa unabii kuzaliwa kwa Yohana

Taarifa ya Jumla

Zakaria na Elizabethi watabulishwa. Mistari hii inatoa taarifa ya historia kuwahusu wao.

Katika siku za Herode, mfalme wa Uyahudi

"Wakati ambao Mfalme Herode alitawala katika Uyahudi"

palikuwa na uhakika

"Palikuwa pa uhakika" au "palikuwa na." Hii ilikuwa njia ya kutambulisha mhusika mpya katika katika historia. Fikiria namna lugha yako inavyofanya.

mgawo

Inafahamika kwamba hii inarejea kwa makuhani. NI: "mgawo wa makuhani au "kundi la makuhani."

wa Abiya

"ambaye alitokea ukoo wa Abiya." Abiya alikuwa mhenga wa kundi la makuhani na wote waliokuwa wanatokea kwa Haruni, ambaye alikuwa kuhani wa kwanza katika Israeli.

"Mke wake alikuwa akitokea katika mabinti wa Haruni."

"Mke wake alitokea ukoo wa Haruni" Hii inamaanisha anatokea katika mfumo ule ule wa kikuhani kama Zakaria. "mke wake pia alitokea pia ukoo wa Haruni" au "Zakaria na mke wake wote wawili walitokea kwa Haruni."

"Kutokea kwa mabinti wa Haruni"

"tokea ukoo wa Haruni"

mbele za Mungu

"mbele za macho ya Mungu" au "kwenye mtazamo wa Mungu"

amri zote na maagizo ya Bwana

"yote ambayo Bwana alishaamuru na aliyotaka"

Lakini

Hili neno la kutofautisha kwamba yafuatayo hapa ni kinyume cha yaliyotarajiwa. watu walitarajia kwamba kama walifanya yaliyosahihi, Mungu angeliwaruhusu kuwa na watoto. Ingawa wanandoa hawa walifanya yaliyo sahihi, hawakuwa na mtoto yeyote.

Luke 1:8

Sasa ikaja kuwa

Hii kauli ilitumika kubadili simulizi kutoka taarifa za mwanzo kwenda kwa wahusika.

katika utaratibu wa mgawo wake

"ilipokuwa zamu ya kundi lake" au "wakati ulipowadia wa kundi lake kuhudumu"

kutokana na desturi ya kuchagua kuhani yupi ambaye ... achome ubani

Sentensi hii inatupa sisi taarifa kuhusu wajibu wa kikuhani.

taratibu za kidesturi

"mfumo wa kiutamaduni" au "njia yao ya kawaida"

kuchagua kwa kura

kura ilikuwa ni jiwe lenye alama ambalo lilitupwa au viringishwa chini ili kwamba liwasaidie kuamua jambo fulani. Makuhani waliamini kwamba Mungu aliielekeza kura kuwaonesha kile walichokitaka makuhani kuchagua.

hivyo anaweza kuchoma ubani

Makuhani walikuwa wanachoma harufu nzuri kama sadaka kwa Mungu kila asubuhi na jioni katika madhabahu maalumu ndani ya hekalu.

mkutano wote wa watu

"Idadi kubwa ya watu" au "Watu wengi"

nje

Kiwanja ilikuwa ni eneo linalolizunguka hekalu. NI: "nje ya jengo la hekalu" au "kwenye kiwanja nje ya hekalu."

katika wakati

"kwenye muda uliopangwa." Haikowazi kama ilikuwa muda wa asubuhi au jioni kwaajili ya sadaka ya ubani.

Luke 1:11

Sentensi Unganishi:

Wakati Zakaria anafanya wajibu wake hekaluni, malaika anakuja kutoka kwa Mungu kumpa ujumbe.

Sasa

Neno hili linazingatia mwanzo wa kitendo katika historia,

alimtokea

"ghafla alikuja kwake" au "ghafla alikuwa pale pamoja na Zakaria." Hii inaweka wazi kwamba malaika alikuwa pamoja na Zakaria, na siyo tu maono.

Zakaria ... alikuwa katekewa ... woga ukamwangukia

Hizi kauli mbili zinamaana ileile, na zinasisitiza jinsi Zakaria alivyokuwa na hofu.

Zakaria alipomuona

"Zakaria alipomwona malaika" Chanzo cha hofu kilikuwa kushituliwa na ile asili ya malaika. Zakaria hakufanya kitu chochote kibaya.

Hofu ikaja juu yake

Hofu ni kitu kinachofafanuliwa kama kwamba shambulio au Zakaria alizidiwa nguvu.

Usiogope

"usiendelee kuniogopa mimi" au "Wewe hutakiwi kuniogopa mimi"

maombi yako yamesikiwa

"Mungu amesikia ambacho uliomba." Kinachofuata kinadokeza na kingeliongezwa: "ataruhusu hiyo." Mungu hakukomea kusikia tu alichoomba Zakaria; pia alikuwa anaelekea kutenda.

utazaa mwana

"mwana wa kiume kwaajili yako" au "kuzaa mtoto wako wa kiume"

Luke 1:14

Kwaajili

"Kwasababu" au "Katika nyongeza kwa hili"

shangwe na kufurahia

Haya maneno mawili yanamaanisha jambo lilelile na yangeliweza kuunganishwa kama lugha haina maneno yanayofanana. NI: "furaha sana."

kwa kuzaliwa kwake

"kwasababu ya kuzaliwa kwake"

atakuwa mkuu mbele ya macho ya Bwana

"atakuwa mtu mhimu sana kwaajili ya Bwana" au "Mungu atamstahilisha kuwa mtu mhimu sana" (UDB)

atajazwa na Roho Mtakatifu

Hii itatajwa kama kauli tendwa: NI: "Roho Mtakatifu atamwezesha" au "Roho Mtakatifu atamwongoza." Hakikisha haieleweki sawa na ambavyo roho mchafu anaweza kumfanya mtu.

toka tumboni mwa mamaye

watu tayari walishawahi kujazwa na Roho Mtakatifu, lakini hakuna hata mmoja aliyesikia mtoto ambaye hajazaliwa kajazwa na Roho Mtakatifu.

Luke 1:16

Watu wengi wa Israeli

Inaeleweka kama japo Zakaria haikuwekwa, kauli hii ingelitafsiriwa kama "wengi wa koo za Israeli" au "wengi wenu ambao ni watu wa Mungu, Israeli." Kama mabadiliko haya yakifanyika, hakikisha kwamba "Mungu wao" imebadilishwa kuwa "Mungu - wao (wingi)."

kurudi

"kirudi nyuma" au "rejea"

atakwenda mbele ya uso wa Bwana

Yeye angelitangulia kutangaza kwa watu kwamba Bwana angelikuja kwao.

mbele ya uso wa

"uso wa" iko hapa ni nahau ambayo inarejea kwenye ule uwepo wa Bwana. Wakati mwingine iliondolewa kwenye tafsiri. NI: "kabla."

katika roho na nguvu ya Eliya

"pamoja na ile roho na nguvu alizokuwa nazo Eliya." Neno "roho" liwe linarejea kwa Roho Mtakatifu wa Mungu au mwenendo wa Eliya au namna ya kufikiri. Hakikisha kwamba neno "roho" halimaanishi mzimu au roho mchafu.

badilisha mioyo baba kuwaelekea watoto

"Kushawishi baba kutunza watoto wao tena" au "kuwasababisha baba kurejesha uhusiano na watoto"

rejesha mioyo

"kurejesha moyo" ni sitiari kwaajili ya kubadili nia ya mtu fulani kuelekea hali fulani.

asiyetii atatembea

"tembea" ni sitiari kwa namna mtu anaishi na kutenda. NI: "asiyetii atatenda" au "asiyetii ataishi"

asiyemtii

"watu ambao hawatii"

fanya tayari kwaajili ya Bwana

haijasemwa jinsi watakavyo kuwa tayari. Hii ilidokeza taarifa zingeliongezwa. NI: "jitayarishe kuamini ujumbe wa Bwana" au "uwe tayari kumtii Bwana."

Luke 1:18

Namna gani naweza kujua hili?

"Jinsi gani naweza kujua kwa hakika kwamba ulichosema kitatokea"? "kujua" kunamaanisha kujifunza kupitia uzoefu, akipendekeza Zakaria alikuwa akiuliza kutokana ishara kama uthibitisho. Hii inaweza kusemwa wazi kama: NI: "unaweza kufanya nini kuthibitisha kwangu kwamba hiki kitatokea?"

Mimi ni Gabrieli, ambaye nasimama katika uwepo wa Mungu

Hii inasemwa kama kukemewa kwa Zakaria. Uwepo wa Gabrieli, unakuja moja kwa moja kutoka kwa Mungu, itakuwa inatosha kumthibitishia Zakaria.

ambaye husimama

"ambaye hutumika"

nilitumwa kuzungumza na wewe

Hii inaweza. kusemwa kwenye mtindo wa kutenda. NI: "Mungu alinituma kusema kwako."

tazama

Neno "tazama" hapa linatutaarifu kuwa makini kwa taarifa zinazofuata za ku.shangaza

ukimya, kutoweza kuzungumza

Hii inamaanisha kitu kilekile, na vilirudiwa kusisitiza ukamilifu wa ukimya wake. NI: "kutoweza kuzungumza kabisa" au "hawezi kuzungumza kwa vyovyote."

kutoamini maneno yangu

"usiamini yale niliyosema"

kwa wakati sahihi

"kwa wakati ulioandaliwa"

Luke 1:21

Sasa

Hii inadokeza kuhama katika simulizi kutokana nakilichotokea ndani ya hekalu kwenda kilichotokea nje. NI: "Wakati huo" au "Wakati malaika na Zakaria wanazungumza."

Walitambua kwamba alishapata maono wakati akiwa hekaluni. Aliendelea kuwafanyia ishara na alibaki kimya.

Mambo haya huenda yalitokea muda uleule, na ishara za Zakaria ziliwasaidia watu kuelewa kwamba amepata maono. Inaweza ikawa msaada kwa wasikilizaji wako wabadili utaratibu kuonesha hivyo. NI: "Yeye aliendelea kuwafanyia ishara na alibaki kimya. Hivyo walitambua kwamba alipata maono wakati akiwa ndani ya hekalu."

maono

maelezo yaliyotangulia yanaashiria kwamba Gabrieli alikuja kweli kwa zakaria hekaluni. Watu, hawajui hilo, walidhani Zakaria aliona maono.

ilitokea

Kauli hii inahamisha simulizi kwenda mbele ambapo huduma ya Zakaria ilikuwa inaishia.

alikwenda nyumbani kwake

Zakaria alikuwa haishi Yerusalemu, ambapo palikuwa na hekalu. Alisafiri kwenda kwenye mji alioishi.

Luke 1:24

Baada ya siku hizi

Kauli "siku hizi" inarejea wakati Zakaria alikuwa anatumika hekaluni. Hii inawezekana kulisema hili kwa uwazi. NI: "Baada ya Zakaria kurudi nyumbani tokea kwenye huduma hekaluni."

mke wake

"mke wa Zakaria"

alijitenga mwenyewe

"hakuondoka nyumbani kwake" au "alibaki peke yake ndani"

Hiki ndicho alichokifanya Bwana kwaajili yangu

Kauli hii inarejea ukweli kwamba Bwana alimruhusu apate ujauzito.

hiki ndicho

Hili ni tamko zuri la mshangao. Yeye alikuwa na furaha sana kwa kile alichokitenda Bwana kwaajili yake.

aliniangalia mimi kwa upendeleo

"Kuangalia" ni nahau ambayo inamaanisha "kutendea" au "kushughulikia." NI: "tazama kwa wema" au "alinihurumia"

aibu yangu

Hii inarejea kwenye aibu aliyoihisi kwa sababu alikuwa hawezi kuwa na watoto.

Luke 1:26

Taarifa kwa Jumla

Malaika Gabrieli anamtangazia Mariamu kwamba anakwenda kuwa mama wa mtu ambaye ni Mwana wa Mungu.

kwenye mwezi wake wa sita

"katika mwezi wa sita wa mimba ya Elizabeth." Hii ilikuwa lazima kulisema wazi kama ingelichanganya na mwezi wa sita katika mwaka.

malaika Gabrieli alikuwa katumwa kutokea kwa Mungu

Hii inaweza kusemwa kwenye mtindo wa kutenda: NI: "Mungu alimwambia malaika Gabrieli nenda"

Yeye ni wa nyumba ya Daudi

"Yeye niwa kabila lilelile kama Daudi" au "Yeye alikuwa ukoo Mfalme Daudi" (UDB)

kaposwa

"rehani" au "kuahidiwa kuolewa." wazazi wa Mariamu waliweka msimamo kwaajili yake atamwoa Yusufu.

jina la bikra alikuwa Mariamu

Hii inamtambulisha Mariamu kama mhusika mpya katika simulizi.

Alikuja kwake

"Malaika alikuja kwa Mariamu"

Salaamu

Hii ilikuwa ni salamu ya kawaida. Inamaana: NI: "furahia" au "uwe na furaha."

ninyi ambao mnaupedeleo mkubwa

"ninyi ambao mmepokea neema kubwa!" au "ninyi mmepokea wema maalumu!"

Bwana yuko pamoja na wewe

"pamoja nawe" ni nahau ambayo inadokeza kutiwa moyo na kukubalika. NI: "Bwana kafurahishwa na wewe."

alikuwa na wasiwasi sana ... salamu hii ingekuwa ya aina gani.

Mariamu alifahamu maana ya maneno hayo, lakini hakuelewa kwanini malaika alimwambia salaamu hii ya kushangaza.

Luke 1:30

Usiwe na hofu, Mariamu

Malaika hakutaka Mariamu kuwa na woga kwa ujio wake, kwasababu Mungu alimtuma ujumbe mzuri.

umepata wema wa Mungu

Nahau "kupata fadhila" inamaana kupokelewa vizuri na mtu fulani. Sentensi inaweza kugeuzwa kuonesha Mungu kama mtenda. NI: "Mungu ameamua kutoa neema yake" au "Mungu anaonesha wema wake."

utakuwa na ujauzito tumboni mwako na kuzaa mwana ... Yesu ... Mwana wa aliye Juu Sana

Mariamu atazaa "mwana" atakayeitwa "Mtoto wa aliye Juu Sana" (UDB). Yesu ni mtoto aliyezaliwa na mama mwanadamu, na Yeye vilevile ni Mwana wa Mungu. Maneno haya yatafsiriwe kwa uanglifu sana.

ataitwa

Maana zinazowezekana ni 1) "watu watamwita" au 2) "Mungu atamwita."

Mwana wa aliye Juu Sana

Hii ni sifa mhimu kwa Yesu, Mwana wa Mungu.

Kupewa kiti cha mhenga wake Daudi

Kiti kinawakilisha mamlaka ya mfalme kutawala. NI: "kumpa mamlaka kutawala kama mfalme kama baba yake Daudi alivyofanya"

hapatakuwa na mwisho kwa ufalme wake

Kauli hasi ""hakuna mwisho" sisitiza kwamba utaendelea milele. Pia inaweza kusemwa kwa kauli chanya. NI: "ufalme wake hautaisha."

Luke 1:34

Namna gani hili litatokea

NI: "Hili linawezekana kwa namna gani?" Ingawa Mariamu hakuelewa jinsi itakavyotokea, yeye hakuwa na shaka kwamba ingelitokea.

Mimi sijalala pamoja na mwanaume yeyote

Mariamu alitumia hali halisi kusema kwamba hajawahi kuhusika kwenye tendo la ngono. NI: "Mimi ni bikra" (UDB)

Roho Mtakatifu atakuja juu yako

utungaji mimba wa Mariamu ungelianza na ujio wa Roho Mtakatifu kwake.

atakuja juu

"kuja ghafla" au "atakutokea"

nguvu ya aliye Juu Sana

Ilikuwa ni nguvu ya Mungu ingelikuja zaidi ya kawaida kumsababisha Mariamu kuwa mjamzito hata wakati akiwa bado akabaki bikra. Hakikisha hii haidokezi hali au muungano wa ngono - huu ulikuwa muujiza.

itakuja juu yako

"utafunikwa kma kivuli"

mtakatifu

"mtoto mtakafu" au "mtoto mchanga mtakatifu"

atakuwa akiitwa

Maana zinazowezekana 1)"watu watamwita" au 2) Mungu atamwita

Hivyo mtakatifu atakayezaliwa ataitwa Mwana wa Mungu

Ingawaje mama yake Yesu alikuwa mwanadamu, Mungu zaidi ya kawaida alimweka Yesu tumboni mwake. Hivyo basi, Mungu alikuwa Baba yake, na Yesu alikuwa anaitwa "Mwana wa Mungu."

Mwana wa Mungu

Hii ni sifa mhimu kwaajili ya Yesu.

Luke 1:36

Na anglia

Huu udhihirisho hapa unasisitiza umhimu wa kauli inayomhusu Elizabeth ambayo inafuata.

ndugu yako Elizabeth

Kama unataka kusema uhusiano maalumu, Elizabeth huenda alikuwa shangazi wa Mariamu au shangazi - mkubwa.

pia anaujauzito wa uzeeni mwake

"pia anaujauzito, ingawa tayari kazeeka, pia mjamzito na atazaa mtoto." Hakikisha haieleweki kama ingawa wawili Mariamu na Elizabethi walikuwa wazee walipopata ujauzito.

mwezi wa sita kwake

"mwezi wa sita wa ujauzito wake"

Kwaajili

Kwa sababu" au "Hii inaonesha hivyo"

hakuna lisilowezekana kwa Mungu

Kauli yake inamashaka maradufu inaweza kutamkwa kwa kauli chanya. NI: "Hii inaonesha Mungu anaweza kufanya kitu chochote." Ujauzito wa Elizabethi ulithibitisha kwamba Mungu anaweza kufanya lolote - hata kumwezesha Mariamu kuwa mjamzito bila kushiriki na mwanaume.

Tazama

Mariamu anatumia udhihirisho huo huo kama malaika kusisitiza jinsi alivyokuwa anajali kuhusu uamzi wake kujikabidhi kwa Bwana.

Mimi ni mtumishi wa kike wa Bwana

Chagua udhihirisho ambao unaonesha unyenyekevu na utii kwa Bwana. Yeye alikuwa hajiinui juu ya kuwa mtumishi wa Bwana.

Acha hii itokee kwangu

"Acha hii itokee kwangu." Mariamu alikuwa anadhihirisha utayari wake kwa mambo yatakayo tokea kwamba malaika alishamwambia yalikuwa karibu yatokee.

Luke 1:39

Sentensi Unganishi

Mariamu anakwenda kumtembelea ndugu yake Elizabethi ambaye alikuwa anakaribia kumzaa Yohana.

aliinuka

Nahau hii inamaanisha hakusimama tu, lakini pia "alikuwa tayari." NI: "alianza kutoka" au "alikuwa tayari"

nchi ya vilima

"eneo la vilima" au "sehemu ya milima ya Israeli"

Alikwenda

Hii inadokeza kwamba Mariamu alimaliza safari yake kabla ya kwenda nyumbani kwa Zakaria. Hii ingelisesemwa wazi. NI: "Yeye alipofika, alikwenda."

Sasa ilitokea

Kauli ilitumika kuonesha tukio jipya katika sehemu ya simulizi hii.

Katika tumbo lake

"katika tumbo la Elizabethi"

karuka

"sogea ghafla"

Luke 1:42

alipaza sauti ... lisema kwa nguvu

Kauli hizi mbili zinamaanisha kitu kilekile, na zinatumika kusisitiza namna Elizabethi alivyokuwa kasisimka. Zingeliweza kuwekwa katika kauli moja. NI: "liotamka ghafla kwa sauti." (UDB)

alipaza sauti yake

Nahau hii inamaanisha "aliongeza kiwango cha sauti yake"

umebarikiwa kati ya wanawake

Nahau "kati ta wanawake" inamaana "zaidi kuliko wanawake wengine."

matunda ya tumbo lako

Mtoto wa Mariamu analinganishwa na matunda ya mti unaozaa. NI: "mtoto katika tumbo lako" au "mtoto utakayemzaa" (UDB)

Na kwa nini hii imetokea kwangu kwamba mama wa Bwana wangu aje kwangu?

Elizabethi alikuwa haulizi apate taarifa. Alikuwa anaonesha jinsi alivyoshangaa na alivyokuwa na furaha kwamba mama wa Bwana amekuja kwake. NI: "Jinsi ilivyokuwa ajabu kwamba mama wa Bwana amekuja kwangu!"

mama wa Bwana

Hii inarejea kwa Mariamu. "wewe, mama wa Bwana wangu." (UDB)

Tazama

Kauli hii inatuamsha tusikilize kushangaa kwa kauli ya Elizabethi inayofuata.

aliruka kwa furaha

"lisogea ghafla kwa furaha" au "ligeuka kwa haraka kwa sababu alikuwa na furaha!"

ilikuja masikioni mwangu

Hii nahau inamaana "nilisikia."

"amebarikiwa yeye ambaye kaamini

"ninyi mlio amini mmebarikiwa" au "kwa sababu mliamini, mtakuwa na furaha"

pale pangekuwa na utimilifu wa mambo

"mambo haya yangelitokea kweli" au "mambo haya yangelikuwa kweli"

mambo ambayo yalisemwa kutoka kwa Bwana kwake

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. " ujumbe ambao Bwana amempa" au "mambo yale uliyo ambiwa na Bwana"

Luke 1:46

Maelezo kwa ujumla:

Mariamu anaanza wimbo wa kumsifu Bwana Mwokozi wake.

Nafsi yangu inasifu ... roho yangu inashangilia

Mariamu anatumia mtindo wa ushairi pale anaposema mambo yale yale katika njia mbili mhimu. ikiwezekana tafsri haya katika tofauti ndogo ya maneno au kauli ambayo inamaana inayofanana.

Nafsi yangu ... roho yangu

Yote "nafsi" na "roho" ... hurejea kwenye viungo vya kiroho vya mtu. Mariamu anasema kwamba ibada yake inatokea kwenye mtima wake wa ndani. NI: "utu wangu wa ndani ... moyo wangu" au "Mimi ... Mimi."

imefurahi ndani

"amehisi kufurahi sana" au "alikuwa na furaha sana"

Mungu Mwokozi wangu

"Mungu, ambaye ndiye aniokoaye mimi" au "Mungu ananiokoaye mimi"

Luke 1:48

Kwa yeye

"Kwa sababu yeye"

alitazama pale

"alitazama pale kwa makini" au "alijali"

hali ya chini

"umaskini." Familia ya Mariamu ilikuwa siyo tajiri.

Angalia

Kauli hii inatoa wito kwa kauli inayofuata.

tokea sasa na kuendelea

"sasa na badaye"

vizazi vyote

"watu wote katika vizazi vyote"

yeye ambaye anauweza

"Mungu, mwenye nguvu" (UDB)

jina lake

Hapa "jina" hurejea kwenye hali yote ya Mungu. NI: "Yeye."

Luke 1:50

Rehema Yake

"rehema ya Mungu"

tokea kizazi kwenda kizazi

"kutoka kizazi kimoja kwenda kizazi kinachofuata" au "kupitia kila kizazi" au "kwa watu wa kila majira"

alionesha nguvu kwa mkono wake

"mkono wake" ni lugha picha inayorejea mkono wa nguvu wa Mungu. NI: inaonesha kwamba Yeye ananguvu sana."

tawanyika

"fukuza katika uelekeo mbalimbali"

mawazo ya mioyo yao

"moyo" ni nahau ambayo inarejea kwenye mawazo ya mtu ya ndani. NI: "mawazo katika utu wao wa ndani."

Luke 1:52

amewashusha chini wafalme kutoka kwenye enzi zao

Enzi ni kiti ambacho mtawala anakalia, na ni mfano wa mamlaka. Kama mfalme akiondolewa kwenye enzi yake, inamaanisha hana mamlaka tena ya kutawala. NI: "Yeye amechukua mamlaka ya wafalme au "watawala kuacha kutawala."

amewashusha chini wafalme ... amewainua juu wenye hali ya chini

Kupingana kati ya hali hizi mbili iwekwe wazi katika tafsiri kama inawezekana.

hali ya chini

"umaskini." Familia ya Mariamu walikuwa siyo tajiri. Angalia livyotafsriwa 1:48.

amewainua ambao wana hali ya chini

Katika neno picha hili, watu ambao ni wa mhimu wako juu zaidi ya wale ambao si mhimu. NI: "amefanya watu wanyenyekevu kuwa wa mhimu" au "amewapa heshima ambao watu wengine hawakuwaheshimu."

amewalisha wenye njaa ... matajiri wameondoka bila kitu

Kutofautisha kati ya matendo wawili yaliyo kinyume itengenezwe tafsiri iliyowazi kama inawezekana.

kashibisha wenye njaa na chakula kizuri

Maana zinazowezekana ni 1) "amewapa wenye njaa chukula kizuri wale" au 2) "kawapa wahitaji vitu vizuri,"

Luke 1:54

Maelezo kwa ujumla

UDB inarekebisha mistari hii kuwa daraja ili kutunza kwa pamoja taarifa zinazohusu Israeli.

ametoa msaada kwa

"Bwana amesaidia"

Israeli mtumishi wangu

Kama wasomaji watachanganya hiki na mtu anayeitwa Israeli, itatafsiriwa kama "mtumishi wake, taifa la Israeli" au "Israeli, mtumishi wake."

Hivyo kama vile

"ili kwamba"

kukumbuka

Mungu hawezi kusahau. Ambapo Mungu "hukumbuka," hii nahau inayomaanisha Mungu anatenda kutokana na ahadi yake aliyotoa mapema.

kama alivyosema kwa baba zetu

"hakika kama alivyoahidi kwa wahenga wetu angelifanya." "Kauli hii inaleta taarifa ya nyuma ahadi ya Mungu kwa Abrahamu." NI: "kwa sababu aliahidi kwa wahenga wetu angelikuwa na rehema."

uzao wake

"wazawa wa Abrahamu"

Luke 1:56

Kauli Unganisha

Elizabethi anajifungua mtoto wake na Zakaria anamwita jina mtoto wao.

alirudi nyumbani kwake

"Mariamu alirudi nyumbani kwake" au "Mariamu alirudi kwenye nyumba yake"

Sasa

Neno hili linaonesha mwanzo wa tukio linalofuata katika historia.

Jirani zake na ndugu zake

"majirani na ndugu wa Elizabethi"

alizidisha rehema yake kwaajili yake

""amekuwa mwema sana kwake" UDB

Luke 1:59

Sasa ilitokea katika hiyo siku ya nane

"Sasa wakati mtoto akiwa na siku nane" au NI: "Ndipo, siku ya nane baada ya mtoto kuzaliwa"

wao

Hii huenda wanarejea kwa Zakaria na rafiki na ndugu wa Elizabethi.

kumtahiri mtoto

Hii ilikuwa sherehe ya kawaida wakati mtu alipokuwa anamtahiri mtoto rafiki zake wapaswa kuwa hapo kusherehekea pamoja na hiyo Familiya. NI: "sherehe kwaajili ya kutahiriwa kwa mtoto."

Wangeliweza kumwita yeye

"Walikuwa wanaenda kumwita yeye" au "Walitaka kumwita yeye jina." Hii ilikuwa desturi ya kawaida.

kama jina la baba yake

"jina la baba yake"

kwa jina hili

"kwa jina hilo" au "kwa jina lilelile"

Luke 1:62

Wao

Hii inarejea kwa watu ambao walikuwa pale kwaajili ya sherehe ya kutahiriwa.

alifanya ishara

"alitaja." Pengine Zakaria alikuwa hawezi kusikia, vilevile kuzungumza, au watu walikisia kwamba hangeliweza kusikia.

kwa baba yake

"kwa baba wa mtoto"

jinsi alivyotaka awe anaitwa

"jina ambalo Zakaria alitaka kumpa mtoto"

Baba yake aliomba ubao wa kuandikia

Inaweza ikasaidia kusema jinsi Zakaria "alivyoomba," Sababu hakuweza kuzungumza. NI: "Baba yake alitumia mikono kuwaonesha watu kwamba alihitaji wampe ubao wa kuandikia"

ubao wa kuandikia

"kitu fulani unachoweza kuandika"

alistaajabishwa

"shangaa sana" au "stajaabishwa"

Luke 1:64

kinywa chake kilifunguliwa ... ulimi wake uliwekwa huru

Hizi kauli mbili ni maneno picha ambayo pamoja yanasisitiza kwamba Zakaria aliweza kuzungumza ghafla.

kinywa chake kilifunguliwa na ulimi wake uliwekwa huru

Kauli hizi zinaweza pia kusemwa katika mtindo wa kutenda. NI: Mungu akafungua kinywa chake na kuuweka huru ulimi."

Hofu ikawajia wote ambao waliishi karibu nao

"Wote walioishi karibu na Zakaria na Elizabethi walikuwa na hofu." Walikuwa wamepigwa butwaa kwa njia ya Mungu ya miujiza kumrejeshea Zakaria uwezo wa kuzungumza. NI: "Kila mmoja aliyeishi karibu nao walikuwa katika hofu ya Mungu."

wote ambao waliishi

Hii hairejei tu kwa wale majirani wa karibu lakini kwa kila mmoja ambaye aliishi eneo hilo.

wote waliowasikia wao

Neno "wao" hapa linarejea kwenye mambo yaliokwisha tokea.

wote waliosikia

Hii inarejea kwenye kundi kubwa la watu walioishi Uyahudi yote.

kusema

"kuuliza"

Mtoto huyu atakuja kuwa kuwa nani?

"Aina gani ya ukuu ambao atakuwa nao mtoto huyu akikua?" Hii pia inawezeakana kwamba swali hili lilikuwa linamaanisha kuwa ni kauli ya kuwashangaza kwa kile walichisikia kuhusu mtoto. NI: "Mtoto huyu atakuwa mkuu wa namna gani!"

mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye

Kauli hii "mkono wa Bwana" inarejea nguvu za Mungu. "Nguvu za Mungu zilikuwa pamoja naye" au "Mungu alikuwa anafanya kazi ndani yake kwa nguvu."

Luke 1:67

Kauli Unganisha:

Zakaria anasema kilichotokea kwa Yohana mtoto wake.

Zakaria Baba yake alikuwa kajazwa na Roho Mtakatifu

Hii inaweza kusemwa kwenye mtindo wa kutendea. NI: "Roho Mtakatifu alimjaza Zakaria baba yake."

Baba yake

baba wa Yohana

alitoa unabii, akisema

fikiria njia za asili za kuanza kunukuu moja kwa moja katika lugha yako. NI: "alitoa unabii na alisema" au "alitoa unabii na hiki ndicho alichokisema"

Mungu wa Israeli

"Israeli" hapa anarejea kwa taifa la Israeli. Uhusiano kati ya Mingu na Israeliungelisemwa moja kwa moja. NI: "Mungu ambaye anatawala juu ya Israeli" au "Mungu ambaye Israeli anamwabudu."

watu wake

"watu wa Mungu"

Luke 1:69

pembe ya wokovu kwaajili yetu

pembe ya mnyama ni mfano kwaajili ya nguvu zake kujitetea yenyewe. Maana hii isemwe wazi. NI: "mtu fulani mwenye nguvu kutuokoa sisi."

ndani ya nyumba ya mtumishi wake Daudi

"Nyumba" ya Daudi inawasilisha familia yake, hasa, ukoo wake, NI: "katika familia ya mtumishi wake Daudi" au "ambaye ni ukoo wa mtumishi wake Daudi"

kama alivyosema

"kama tu Mungu alivyosema"

alisema kwa kinywa cha manabii wake watakatifu

Mungu aliwawezesha manabii kuzungumza neno alilotaka wao wazungumze. udhibiti wa Mungu unaweza kusemwa NI: "alisababisha manabii wake watakatifu kusema."

kwa mdomo wa

Hii inazungumzia ujumbe wa manabii kama ilikuwa midomo inasema maneno NI: "kwenye maneno ya"

walikuwapo katika ulimwengu wa kale

"waliishi zamani"

kuleta wokovu

Hii inarejea kwenye wokovu wa mwili, zaidi kuliko wokovu wa kiroho.

adui zetu ... wote wanaotuchukia

Hizi kauli mbili kimsingi zinamaanisha jambo lilelile na zimerudiwa kusisitiza jinsi adui zao walivyokuwa na nguvu kinyume chao.

kutoka katika mkononi mwa

Itakuwa ni msaada kusema tena "wokovu" hapa. NI: "wokovu kutokana na mkono wa."

mkono

"nguvu" au "udhibiti." Neno "mkono" linakwenda pamoja na nguvu ambazo zinatumika kuwaumiza watu wa Mungu

Luke 1:72

kuonesha rehema

"kuwa na huruma kwa" au "kutenda kutokana na rehema yake kwao"

kumbuka

Hapa neno "kumbuka" linamaana kuendelea kujitoa au kukamilisha kitu fulani.

agano lake takatifu ... kiapo ambacho alikisema

Kauli hizi mbili zinarejea kwenye kitu kile kile. Zimerudiwa kuonesha kujali kwa Mungu juu ya ahadi kwa Abrahamu.

kutoa idhini kwetu

"kufanya iwezekane kwaajili yetu"

kwamba sisi, tumekombolewa ... tumtumikie yeye bila hofu

Inaweza ikasaidia kubadili mtindo wa kauli hizi. NI: "kwmba tungelimtumikia yeye bila bila hofu baada sisi kuokolewa kutoka katika nguvu za adui wetu."

kutoka katika mkono wa adui zetu

"mkono" inarejea kudhibiti au nguvu ya mtu. Hii inaweza kusemwa wazi. NI: "kutoka katika udhibiti wa adui zetu."

bila hofu

Hii inarejerea nyuma kwenye hofu ya adui zao. NI: "bila kuwaogopa adui zetu"

katika utakatifu na haki

Hizi zinaweza kudhihirishwa kama matendo. NI: "kuishi katika njia safi na kutenda haki"

mbele yake

Nahau hii ambayo inamaanisha "katika uwepo wake"

Luke 1:76

ndiyo, na wewe

Zakaria anatumia kauli hii kuanza hotuba yake moja kwa moja kwa mtoto wake. Unaweza kuwa na njia ile ile ya kuhutubia moja kwa moja katika lugha yako.

huyu, mtoto, ataitwa nabii

Watu watatambua kwamba huyu ni nabii. Hii inaweza ikasemwa katika mtindo wa kutendea. NI: "watu watajua kwamba wewe ni nabii."

wa aliye Juu Sana

"ambaye anamtumikia aliye Juu Sana." Hii inarejea kwa Mungu. NI: "ambaye anazungumza kwaajili ya Mungu aliye Juu Sana."

kwenda mbele za uso wa Bwana

Nahau hii inamaana "kwenda mbele za Bwana" au "kuja mbele za Bwana."

kuwapa maarifa ya wokovu watu wake

"kuelezea wokovu kwa watu wake" au "hivyo watu wake waweze kufahamu wokovu"

kwa msamaha wa dhambi zao

"kupitia msamaha wa dhambi zao." Pia inaweza kusemwa katika mtindo wa kutendea. NI: "kwa sababu Mungu amewasamehe"

Luke 1:78

Maelezo kwa ujumla

Kupitia katika mistari hii : "sisi" inahusisha watu wote.

kwa sababu kawaida ya huruma iliyotolewa na Mungu wetu

Hii inaweza kusaidia kusema kwamba rehema ya Mungu inatusaidia sisi. NI: "kwa sababu Mungu anahuruma na na rehema kwetu."

jua linachomoza kutoka juu ... kuchomoza juu

Mwanga kwa kawaida ni sitiari kwa ukweli. Hapa, jinsi jua linavyochomoza mwanga wake juu ya nchi ilitumika kama mfano wa jinsi mwokozi anavyotoa ukweli wa kiroho kwa watu.

angaza juu

"toa maarifa kwa" au "toa mwanga wa kiroho kwa"

wao wanaokaa gizani

Giza hapa ni sitiari kwa watu wasio na kweli. Hapa, watu ambao wanapungukiwa ukweli wa kiroho wanasemwa kama kwamba wanakaa gizani. NI: "watu wasiojua kufanya kweli"

giza... kivuli cha kifo

kauli hizi mbili zinafanya kazi pamoja kusisitiza giza nene la kiroho kwa watu Mungu huwaonesha rehema kwao.

katika kivuli cha mauti

kivuli ni sitiari kwa kitu fulani ambacho kinakabili. Hapa, inarejea kwenye giza la kiroho ambalo litawasababisha kufa. NI: "ambao wanakaribia kufa."

ongoza miguu yetu

Kuongoza mtu kutembe ni sitiari ya kuongoza ufahamu wa kiroho. NI: "tuongoze" au "Tufundushe."

miguu yetu

"miguu" inatumika kuwakilisha mtu kwa ujumla. NI: "sisi"

katika njia ya amani

"njia ya amani" ni sitiari kwaajili ya njia inayomsababisha mtu kuwa na amani na Mungu. NI: "kuishi maisha ya amani" au "kutembea katika njia ambayo inatuongoza kwenye amani."

Luke 1:80

Maelezo kwa ujumla:

Hii inatuambia kwa kifupi kuhusu miaka ya Yohana kuongezeka.

Sasa

Neno hili linatumika hapa kuonesha kituo kwenye mfululizo wa habari kuu. Luka anahama kwa haraka kutoka kuzaliwa kwa Yohana kwenda kwenye huduma yake.

kuwa na nguvu katika roho

"kukomaa kiroho" au "kuimarisha uhusiano na Mungu"

alikuwa katika mwitu

"aliishi katika mwitu." Luka hasemi katika umri gani Yohana alianza kuishi mwituni.

mpaka

Hii siyo lazima kuonesha hoja ya kumalizia. Yohana anaendelea kuishi katika pori hata baada ya kuanza kuhubiri hadharani.

siku ya kujitokeza kwake

"alipoanza kuhubiri hadharani"

siku

Hii ilitumika hapa katika dhana ya jumla ya "wakati" au "fursa"

Luke 2

Luka 02 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri hupendelea kuweka sala ndefu au unabii mbele kidogo ya maandiko nyingine. Kwa sababu hii, ULB na tafsiri nyingine nyingi za Kiingereza huingiza mistari ya 2:14, 29-32.

"Dhana maalum katika sura hii"

Hakukuwa na nafasi kwao

Maelezo ya Luka kuhusu kuzaliwa kwa Kristo hauna maelezo mengi kama vile injili nyingine. Huenda Luka hakufikiri kama maelezo haya yalikuwa muhimu, labda kwa sababu ya habari za kuzaliwa katika injili nyingine.

<< | >>

Luke 2:1

Maelezo kwa ujumla

Hii inatoa maelezo ya nyuma kuonesha kwanini Mariamu na Yusufu wanatakiwa kuondoka kwaajili ya kuzaliwa kwa Yesu.

Sasa

Neno hili ni alama ya kuanza kwa sehemu mpya ya simulizi.

ikaja ikawa kwamba

Kauli hii ilitumika kuonesha kwamba huu ni mwanzo wa wajibu. Kama lugha yako inayo njia ya kuonesha kuanza kwa kuwajibika, unaweza ukatumia hiyo. Baadhi ya tafsiri haziweki kauli hii.

Kaisari Agusto

"Mfalme Agusto" au "Mtawala Agusto." Agusto alikuwa mtawala wa kwanza wa dola ya Rumi.

alitoa agizo likielekeza

Amri hii huenda ilinabebwa na wajumbe kupitia katika dola. NI: "wajumbe waliotumwa maelekezo ya amri"

kwamba ichukuliwe sensa ya watu wote wanaoishi katika ulimwengu

Hii inaweza kusemwa katika mtindo wa kutendea. NI: "kwamba waorodheshe watu wote wanaoishi katika ulimwengu wa kirumi" au "wahesabu watu wote katika ulimwengu wa kirumi na waandike majina yao."

ulimwengu

eneo la dunia lililotawaliwa na serikali ya Rumi au "nchi zilizoongozwa na dola ya Kirumi"

Krenio

Krenio aliteuliwa kuwa mtawala wa Siria/Shamu

kila mmoja alikwenda

"kila mmoja aliondoka" au "kila mmoja alikuwa anakwenda"

mji wa kwao

Inaweza ikasaidia kusema kwamba "ya kwake" hairejei kwenye mji ambao alikuwa akiishi. NI: "ni mji ambao wahenga wake waliishi."

kuandikishwa kwaajili ya sensa

"kuwa na majina yameandikwa kwenye orodha" au "kuwekwa kwenye idadi kiofisi"

Luke 2:4

Maelezo kwa ujumla

UDB inaweka sawa hii mistari miwili kuwa daraja ambalo litatengeneza urahisi wa kufupisha sentensi.

pia Yusufu

Hii inamtambulisha Yusufu kama mhusika mpya katika simulizi.

kwenye mji wa Daudi

Taarifa hizi zilizotangulia kuhusu umhimu wa wa Bethlehemu. Ingawa ulikuwa mji mdogo, Mfalme Daudi alizaliwa pale, na ulikuwapo unabii kwamba masihi atazaliwa pale. NI: ambao ulikuwa unaitwa mji wa Daudi"

kwa sababu alikuwa wa nyumba na familia ya Daudi

"kwa sababu Yusufu alikuwa wa uzao wa Daudi"

Kuandikisha

Hii inamaanisha kutaarifu kwa afisa kule hivyo wamhusishe naye kwenye wajibu. Tumia kauli kwaajili ya afisa mwandikishaji wa serikali ikiwezekana.

pamoja na Mariamu

Mariamu alisafiri pamoja na Yusufu kutoka Nazarethi. Ni wazi kwamba wanawake pia walihitajika, hivyo Mariamu angelihitaji kusafiri na kuandikishwa vile vile.

ambaye alikuwa kaposwa naye

"mchumba wake" au "aliyekuwa ameahidi kwake." Wachumba walihesabiwa kisheria wameoana, lakini pale isingelikuwa kukaribiana kimwili kati yao.

Luke 2:6

Kauli Unganishi:

Hii inatuambia kuzaliwa kwa Yesu kwa tangazo la malaika kwa wachungaji.

Maelekezo kwa ujumla:

UDB inapanga upya mistari hii katika mstari daraja ili kutunza pamoja undani kuhusu mahali walipokaa.

Sasa ikaja kwamba

Kauli hii inaweka alama ya kuanza kwa tukio linalofuata katika simulizi.

wakati wakiwa pale

"wakati Mariamu na Yusufu walikuwa Bethlehemu"

wakati ukawadia wa kuzaa mtoto

"ilikuwa ni muda wa kujifungua mtoto wake"

alimsetiri kwa nguo nadhifu

Hii ilikuwa ni njia ya kawaida kwa akinamama kukinga na kutunza watoto wao kiutamaduni. ungesema hii wazi: NI: "akasetiri joto kwa kumfunga blanketi vizuri" au "akamfunga kumsetiri kwa blanketi."

alimlaza katika kihori

Hiki kilikuwa aina ya kiboksi au chombo ambacho watu waliweka nyasi kavu au chakula kingine ndani yake kwaajili ya chakula cha wanyama. kilikuwa safi sana na kilikuwa laini na kavu kama nyasi kavu ndani kama sponji kwa mtoto. Wanyama kawaida walitunzwa karibu na nymbani kuwalinda kiusalama na kuwalisha kwa urahisi. Ni dhahiri Mariamu na Yusufu walibaki kwenye eneo ambalo lilitumika kwaajili ya wanyama.

hapakuwa na nafasi kwaajili yao katika nyumba za wageni

"hapakuwa na mahali kwaajili yao kwenye vyumba vya wageni." Hii huenda ilikuwa kwa sababu ya watu wengi walikwenda Bethlehemu kujiandikisha. Luka anaongeza kama taarifa ya iliyokwishakutolewa.

Luke 2:8

Malaika wa Bwana

""malaika kutoka kwa Bwana" au "malaika anayemtumikia Bwana"

aliwatokea

"akaja kwa wachungaji"

utukufu wa Bwana

chanzo cha mwanga mweupe ulikuwa ni utukufu wa Bwana, ambao uliwatokea kwa wakati ule ule kama malaika.

Luke 2:10

usiwe na hofu

"koma kuwa na hofu"

kwamba zitaleta furaha kwa watu wote

"kwama zitawafanya wote kufurahi sana"

watu wote

Baadhi wanafahamu hii kurejea kwa Wayahudi. Wengine wanaelewa inarejea kwa watu wote.

mji wa Daudi

Hii inamaanisha Bethlehemu

Hii ni ishara itakayotolewa kwenu

Hii inaweza kusemwa kwenye mtindo tendea. NI: "Mungu atawapa ishara hii" au "mtaona ishara hii inayotoka kwa Mungu."

ishara

""uthibitisho." Hii pengine inaweza kuwa ishara kuthibitisha kwamba kile ambacho malaika alikuwa anasema ni kweli, au inaweza kuwa ishara ambayo ingelisaidia wachungaji kumtambua mtoto.

atasetiriwa katika nguo nadhifu

Hii ilikuwa njia ya kawaida kwamba mama alimlinda na kutunza watoto wao katika utamaduni huo. NI: "alisetiriwa vema katika blanketi itunzayo joto" au "alifungwa kwaufanisi kwenye blanketi." Angalia jinsi ilivyotafsiriwa 2:2.

Kalala katika kihori cha kulishia

Hiki kilikuwa kiboksi au kitu ambabacho watu waliweka humo majani au chakula kwaajili ya kula ng'ombe. Angalia jinsi ilivyotafsiriwa katika 2:6.

Luke 2:13

idadi kubwa, ya jeshi la mbinguni

Neno "jeshi la mbinguni" hapa itarerejea kwenye jeshi halisi la malaika, au inawezakuwa sitiari kwaajili kikundi cha malaika kilicho andaliwa. NI: "kundi kubwa la malaika kutoka mbinguni." (UDB)

kumsifu Mungu

"kumpa sifa Mungu"

Utukufu kwa Mungu juu sana

Maana zinazowezekana ni 1) "Toa heshima kwa Mungu aliye mahali pa juu sana" au 2) "Toa heshima ya juu sana kwa Mungu."

hapa duniani iweze kuwa amani kati ya watu ambao ameridhishwa nao

"wale watu ambao wako duniani ambao Mungu ameridhishwa nao basi wawe na amani"

Luke 2:15

Ikawa

kauli hii ilitumika kuonesha kubadili kwa masimulizi kwenda kwenye ambacho wachungaji walifanya baada ya malaika kuondoka.

kutoka kwao

"kutoka kwa wachungaji"

Baina ya mtu na mtu

"kwa mmoja na mwingine"

ngoja nasi ... kwetu

Tangu wachungaji walikuwa wanazungumza mmoja na mwingine, lugha ambayo inamtindo wa kuhusisha kwa "sisi" na "nasi" tumia mtindo wa kuhusisha hapa.

ngoja nasi

"nasi tuta"

jambo hili ambalo limetokea

Hii inarejea kuzaliwa kwa mtoto, na siyo kuonekana kwa malaika.

kalala katika kihori cha kulishia

Hii ilikuwa aina fulani ya boksi au kitu ambacho watu waliweka nyasi kavu au chakula kwaajili ya wanyama kula. Angalia jinsi ilivyotafsiriwa katika 2:6.

Luke 2:17

ambacho kilikuwa kimesemwa kwao na wachungaji

Hii inaweza ikasemwa kwenye mtindo wa kutendea. NI: ""kile ambacho malaika waliwaambia wao wachungaji."

mtoto huyu

"mtoto"

kile ambacho kilizungumza kwao na wachungaji

Hii inaweza kusemwa katika mtindo wa kutendea. NI: "ambacho wachungaji waliwaambia."

kuyatunza moyoni mwake

hazina ni kitu fulani ambacho ni cha thamani sana na kizuri. Mariamu alifikiri mambo aliyoambiwa kuhusu mtoto wake kuwa ni mazuri sana. NI: "kuyakumbuka kwa makini" au "kuyakumbuka kwa furaha."

walirudi

"wakarudi mashambani kwenye kondoo"

kumtukuza na kumsifu Mungu

haya yanafanana na yanasisitiza jinsi walivyochangamka kuhusu kile ambacho Mungu kafanya. NI: "sema juu ya kusifu ukuu wa Mungu."

Luke 2:21

Maelezo kwa ujumla:

Sheria Mungu aliyowapa Wayahudi waamini aliwaambia lini mtoto mvulana atahiriwe na sadaka ipi wazazi walete.

ilipokuwa mwishoni mwa siku ya nane

kauli hii inaonesha muda ukapita kabla ya tukio jipya.

mwishoni mwa siku ya nane

"ilikuwa siku nane baadaya kuzaliwa kwake" au "alikuwa na umri wa siku nane"

aliitwa

Yusufu na Mariamu walimwita jina lake.

jina alilokwishakuwa amepewa na malaika

Hii inaweza kusemwa katika mtindo wa kutendea. NI: "jina ambalo malaika alimwita."

Luke 2:22

wakati hesabu iliyotakiwa ... ilishapita

Hii inaonesha kupita kwa muda kabla ya tukio jipya.

hesabu iliyotakiwa ya siku

Hii inaweza kusemwa kwenye mtindo wa tendea. NI: "hesabu ya siku ambazo Mungu alitaka."

kwaajili ya kujitakasa kwao

"kwaajili ya wao kuwa safi kiutaratibu." Pia unaweza kuisema nafasi ya Mungu. "Mungu kutaka wao wawe safi tena."

kumkabidhi kwa Bwana

"kumleta kwa Bwana" au "kumleta yeye kwenye uwepo wa Bwana." Hii ilikuwa ni sherehe kutambua nia ya Mungu kwa mtoto mzaliwa wa kwanza ambaye ni wa kiume.

kama ilivyo andikwa

Hii inaweza kusemwa katika mtindo wa tendea. NI: "kama alivyo andika Musa" au "walifanya hivyo kwa sababu Musa aliandika."

kila mwanaume ambaye anafungua tumbo

"fungua tumbo" ni nahau ambayo inarejea kwa mtoto wa kwanza kutoka tumboni. Hii ilirejea kwa wote wanyama na wanadamu. NI: "kila mzaliwa wa kwanza mtoto ambaye ni mwanaume."

hicho ambacho kilisemwa katika sheria ya Bwana

"ambacho sheria ya Bwana inasema." Hii ni sehemu tofauti katika sheria. Inarejea kwa wanaume, iwe mzaliwa wa kwanza au sivyo.

Luke 2:25

Kauli Unganishi:

Wakati Mariamu na Yusufu wako hekaluni, waliwaona watu wawili: Simeoni, ambaye alimsifu Mungu na kutoa unabii kuhusu mtoto, na nabii mke Ana.

Tazama

Neno "tazama" linatuashiria mtu mpya katika simulizi. Lugha yako inaweza ikawa na njia ya kutenda hivi.

alikuwa mwenye haki na mcha Mungu

Kauli za nadharia hizi zinaweza kudhihirishwa kama matendo. NI: "alifanya kilichokuwa kinamridhisha Mungu na alitii sheria za Mungu."

mfariji wa Israeli

Hili ni jina jingine la "Masihi" au "Kristo." NI: "ndiye ambaye atafariji Israeli."

Roho Mtakatifu alikuwa juu yake

"Roho Mtakatifu alikuwa pamoja naye." Mungu alikuwa pamoja naye katika njia maalumu na alimpa hekima na maelekezo katika maisha yake.

ikafunuliwa kwake na Roho Mtakatifu

Hii inaweza kusemwa katika mtindo tendea. NI: "Roho Mtakatifu akamwonesha" au "Roho Mtakatifu akamwambia."

asingalikufa kabla hajamwona Kristo Bwana

"angelimwona Masihi Bwana kabla hajafa"

Luke 2:27

ikatokea

Baadhi ya lugha zinaweza kusema "kwenda"

aliongozwa na Roho Mtakatifu

Hii inaweza kusemwa katika mtindo tendea. NI: "kama Roho Mtakatifu alivyo mwelekeza."

kwenye hekalu

"katika kiwanja cha hekalu." Makuhani tu wangeliigia kwenye jengo la hekalu.

wazazi

"wazazi' wa Yesu"

desturi ya sheria

"desturi ya sheria ya Mungu"

Sasa mpe ruhusa mtumishi wako aende kwa amani

"Mimi mtumishi wako; niruhusu niende katika amani." Simeoni alikuwa anarejea kwake mwenyewe.

ondoka

Hii ni tasifida imaanishayo "kufa"

kutokana na neno lako

"kama ulivyosema" au "kwasababu ulisema ningeli"

Luke 2:30

macho yangu yameona

Udhihirisho huu unamaanisha, "Nimeona mwenyewe" au "Mimi, Mwenyewe, nimeona"

wokovu wako

Udhihirisho huu unarejea kwa mtu ambaye angeleta wokovu - mchanga Yesu--ambaye Simeoni alikuwa amembeba. NI: "mwokozi ambaye umemtuma" au "yeye ambaye ulimtuma kuokoa" (UDB)

ambacho wewe

inategema na jinsi unavyo tafsiri kauli iliyopita, hii inahitaji kubadilishwa kuwa "ambaye wewe."

umeandaa

"umepanga" au "ulisababisha itokee"

Nuru

Sitiari hii inamaanisha kwamba mtoto atasaidia watu kuona na kufahamu njia inasema mwanga husaidia watu kuona barabara. NI: "huyu mtoto anawezesha watu kuelewa nuru inavyoruhusu kuona barabara."

kwaajili ya ufunuo

iwe lazima kusema ambacho kimefunuliwa. NI: "ambacho kitaufunua ukweli wa Mungu."

Udhihirisho

itakuwa lazima kusema udhihirisho ni nini, NI: "kwamba itadhihirisha ukweli wa Mungu"

utukufu kwa watu wako Israeli

"atakuwa sababu kwamba utukufu utakuja kwa watu wako Israeli"

Luke 2:33

mambo ambayo yalisemwa kumhusu yeye

Hii inaweza ikasemwa katika mtindo wa kutendea. NI: "mambo ambayo Simeoni aliyasema kumhusu yeye."

alimwambia Mariamu mama yake

"alisema kwa mama wa mtoto, Mariamu." Hakikisha haieleweki kama Mariamu ni mama wa Simeoni.

Tazama

Simeoni alitumia udhihirisho huu kumwambia Mariamu kwamba ambacho anachokwenda kukisema ni cha mhimu sana kwake.

mtoto huyu ni mstaakabali wa kuanguka na kuinuka kwa wengi katika Israeli.

Neno "kuinuka" na "kuanguka" yanadhihirisha kugeuka kutoka kwa Mungu na kumkaribia Mungu karibu. "mtoto huyu atasababisha watu wengi katika Israeli kuanguka kutoka kwa Mungu au kuinuka karibu na Mungu."

kwaajili ya ishara ambayo ilikataliwa

"kwaajili ya ujumbe kutoka kwa Mungu kwamba watu wengi watapinga"

upanga utapenya nafsini mwako

Sitiari hii inafafanua huzuni ya ndani ambayo Mariamu angeliisikia. NI: "Huzuni yako itakuwa maumivu ingawa kama upanga utapenya moyoni mwako."

mawazo kutoka kwenye "mioyo" mingi yatadhihirishwa"

NI: "mawazo ya watu wengi yatawekwa wazi."

Luke 2:36

Nabii mke jina lake Ana pia alikuwa pale

Hii inatambulisha mhusika mpya katika simulizi.

Fanueli

"Fanueli" ni jina la mwanaume.

miaka saba

"miaka 7 "

baada ubikra wake

"baada ya kuolewa naye"

mjane kwa miaka themanini na minne

miaka minne - Maana zinazowezekana 1) kawa mjane kwa miaka 84 au 2) alikuwa mjane na alikuwa na umri wa miaka 84.

hakuondoka hekaluni

Hii huenda ni maana iliyokuzwa kwamba alitumia muda mwingi katika hekalu hii ilionekana kama kwamba hakuondoka pale. NI: "kila mara alikuwa hekaluni" au "daima alikuwa hekaluni."

akifunga na kuomba

"kujinyima chakula na maombi"

akawajia karibu yao

"kuwafuata" au "alikwenda kwa Mariamu na Yusufu"

wokovu wa Yerusalemu

Hapa neno "wokovu" lilitumika kurejea kwa mtu ambaye angetenda. NI: yule ambaye angeokoa Yerusalemu" au "mtu ambaye angeleta baraka za Mungu na fadhila tena kwa Yerusalemu."

Luke 2:39

Kauli Unganishi:

Mariamu, Yusufu na Yesu waliondoka Bethlehemu na kurudi kwenye mji wa Nazarethi kwaajili ya utoto wake.

wao walitakiwa kufanya kutokana na sheria ya Bwana

Hii inaweza kusemwa katika mtindo wa kutendea. NI: "kwamba sheria ya Bwana iliwataka kufanya."

mji wa kwao, Nazarethi

Kauli hii inamaana waliishi Nazarethi. Hakikisha haieleweki kama mji ulio milikiwa.

kuongezeka katika hekima

"kuwa na hekima zaidi" au "alijifunza ambayo yalikuwa ya hekima"

neema ya Mungu ilikuwa juu yake

"Mungu alimbariki" au "Mungu alikuwa pamoja naye kwa namna pekee"

Luke 2:41

Kauli Unganisha

Wakati Yesu akiwa na umri wa mika 12, huenda Yerusalemu pamoja na familia yake. Wakati akiwa pale, anauliza na kujibu maswali kwa waalimu hekaluni.

Wazazi wake walikwenda ... sherehe ya Pasaka

Haya ni maelezo ya nyuma. (angalia:

Wazazi wake

"Wazazi wa Yesu"

wakapanda tena

Yerusalemu ulikuwa juu ya mlima zaidi kuliko ya maeneo mengine, hivyo wilikuwa kawaida kwa Waisreli kusema wanapanda kwenda huko Yerusalemu.

kwa muda wa kidesturi

"muda wa kawaida" au "kama walivyofanya kila mwaka"

baada ya kubaki kwa siku nyingi kwaajili ya sherehe

"Wakati wote wa kusherehekea sikuu ulipokwisha" au "Baada ya kusherehekea sikukuu kwa siku zote zilizotakiwa"

sikukuu

Hili ni jina lingine la kwaajili ya sherehe ya Pasaka, sababu ilihusisha kula chakula cha sherehe.

Walidania

"walifikiri"

walisafiri safari ya siku nzima

"walisafiri siku moja" au "walikwenda umbali wa kama watu wanatembea siku moja"

Luke 2:45

ikatokea kwamba

Kauli hii ilitumika hapa kuashiria umhimu wa tukio katika simulizi. Kama lugha yako ina namna ya kufanya hivi, ufikiri kuitumia hapa.

katika hekalu

Hii inarejea kwenye kiwanja cha hekalu. Makuhani tu walioruhusiwa ndani ya hekalu. NI: "katika kiwanja cha hekalu" au "kwenye hekalu."

katikati ya

Hii haina maana ya katikati kabisa. Zaidi, inamaanisha, "kati" au "pamoja na" au "kuzunguka."

waalimu

"waalimu wa dini" au "wale ambao waliwafundisha watu kuhusu Mungu"

wote waliosikia walishangaa

Walikuwa hawawezi kuelewa namna gani mvulana wa miaka kumi na miwili asiye na elimu ya dini ajibu vizuri hivyo.

kwenye ufahamu wake

"kwa kiwango kipi alielewa" au "kwamba yeye anaelewa mengi sana kuhusu Mungu"

majibu yake

"kwa namna alivyo wajibu vizuri" au "kwamba yeye aliwajibu maswali yao vizuri sana"

Luke 2:48

Walipomwona yeye

"Wakati Mariamu na Yusufu wanamwona Yesu"

kwanini umetutendea namna?

Hii ilikuwa kumkemea kwa kupindisha kwa sababu hakwenda pamoja nao wakati wa kurudi nyumbani. NI: usingefanya hivi!"

Sikiliza

Hili neno daima linatumika kuonesha mwanzo wa tukio jipya au mhimu. Hii pia inaweza kuonesha kutumika mahali tukio linapoanzia. Kama lugha yako inakauli ambayo inatumika kwa njia hii, fikiri ikiwa itaonesha uasili ikitumika hapa.

Kwa nini mlikuwa mnanitafuta mimi?

Yesu alitumia maswali mawili kuwakemea wazazi wake kwa upole, na kuanza kuwaambia kwamba analo kusudi kutoka kwa Baba yake wa mbinguni ambalo wao hawakulielewa. NI: "mlikuwa hamhitajiki kunijali mimi."

ninyi hamkujua ... nyumbani?

Yesu anatumia swali hili la pili kujitahidi kusema kwamba wazazi wake wangejua kuhusu kusudi ambalo Baba alimtuma. NI: "Ninyi mngejua ... nyumbani."

Baba yangu

Kwenye miaka 12, Yesu, Mwana wa Mungu, alielewa kwamba Mungu alikuwa Baba yake halisi (siyo Yusufu, mume wa Mariamu).

ndani ya nyumba ya Baba yangu

Maana zinazowezekana ni 1) "katika nyumba ya Baba yangu" au 2) "kuhusu biashara ya Baba yangu." Ikiwa kwa lolote, ambalo Yesu alisema "Baba yangu" alikuwa anarejea kwa Mungu. Kama alimaanisha "nyumba," basi alikuwa anarejea hekalu. Kama alimaanisha "biashara," alikuwa anarejea kwenye kazi ya Mungu aliyopewa kuifanya. Lakini sababu ya mstari unaofuata anasema kwamba wazazi wake hawakuelewa ambacho alichokuwa anawaambia hao, ingelikuwa vema usifafanue zaidi.

Luke 2:51

alirudi nao nyumbani

"Yesu alirudi nyumbani pamoja na Mariamu na Yusufu"

ulikuwa utii kwao

"aliwatii" au "kwa njia zote aliwatii"

alihifadhi mambo yote moyoni mwake

"alikumbuka mambo yote kwa makini" au "kwa furaha alifikiri kuhusu mambo haya." Maneno "kuhifadhi" au "moyo" yanaashiria kwamba Mariamu alijali mambo haya kuwa ni yanamhusu kwa kina na ni mhimu.

kukua katika hekima na kimo

"kuwa na hekima sana na nguvu." Hivi vinarejea kwenye akili na kukua kimwili.

kuongezaka kupata fadhila kwa Mungu na watu

Hii inarejea kukua kiroho na kijamii. Hii ingetofautishwa. NI: "Mungu alimbariki zaidi na zaidi, na watu walimpenda zaidi na zaidi."

Luke 3

Luka 03 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri hupendelea kuweka nukuu mbele kidogo ya maanidko nyingine za Agano la Kale. ULB na tafsiri nyingine nyingi za Kiingereza huingiza mistari ya 3:4-6, ambayo ni nukuu kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

Haki

Maelekezo ya Yohana kwa askari na watoza ushuru katika sura hii si ngumu. Ni mambo ambayo yaliyopaswa kuwa wazi kwao. Aliwaagiza kuishi kwa haki. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#justice and Luke 3:12-15)

Nasaba

Nasaba ni orodha ambayo hurekodi mababu au wazao wa mtu. Orodha hizo zilikuwa muhimu sana katika kuamua nani aliyekuwa na haki ya kuwa mfalme, kwa sababu mamlaka ya mfalme mara nyingi ilipokelewa au kurithiwa kutoka kwa baba yake. Ilikuwa pia ya kawaida kwa mtu yeyote mashuhuri kuwa na kumbukumbu ya kizazi.

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Sitiari

Unabii mara nyingi huhusisha matumizi ya sitiari ili kueleza maana yake. Utambuzi wa kiroho unahitajika kwa tafsiri sahihi ya unabii. Unabii wa Isaya ni sitiari ndefu unaoeleza huduma ya Yohana Mbatizaji (Luka 3:4-6). Tafsiri ni ngumu. Inapendekezwa kuwa mtafsiri azingatie kila mstari wa ULB kama mfano tofauti. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#prophet) and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"(Herode) alimfunga Yohana gerezani"

Tukio hili linaweza kuchanganya kwa sababu mwandishi anasemaYohana alifungwa na kisha anasema alikuwa akibatiza Yesu. Mwandishi huenda anatumia maneno haya kwa kutarajia wakati Herode anamfunga Yohana. Hii inamaanisha kwamba taarifa hii iliandikwa kabla ya tukio lenyewe katika maandishi.

<< | >>

Luke 3:1

Sentensi unganisha

Maelezo kwa Ujumla

Katika mwaka wa kumi na tano wa wa utawala wa Kaisari Tiberio

"Wakati akitawala Kaisari Tiberio ikiwa miaka kumi na tano"

Filipo ... Lisania

Haya ni majina ya watu.

Iturea na Trakoniti...Abilene

Haya ni majina ya maeneo ya utawala

Kipindi cha ukuhani mkuu wa Annasi na Kayafa

"Wakati ambapo Anasi na Kayafa walikuwa wakihudumu pamoja kama kuhani mkuu." Anasi alikuwa kuhani mkuu, na wayahudi waliendelea kumtambua hivyo hata baada ya Warumi walipomteuwa mtoto wake mkwe, Kayafa, kuchukua nafasi yake kama kuhani mkuu.

neno la Mungu likaja

"Mungu alisema neno lake"

Luke 3:3

Akihubiri ubatizo wa toba

Neno "Ubatizo" na "Toba" yanaweza kuelezewa kama vitendo. AT: "na alihubiri kwamba watu wale inapaswa kubatizwa kuonyesha kwamba walikuwa wakitubu."

Kwa ajili ya msamaha wa dhambi

"Ili kwamba dhambi zao zingeweza kusamehewa" au "ili kwamba Mungu angeweza kusamehe dhambi zao." Toba ilikuwa kwamba Mungu aweze kusamehe dhambi zao.

Luke 3:4

Maelezo kwa Ujumla

Mwandishi, Luka, kanukuu mstari kutoka nabii Isaya tokana na Yohana Mbatizaji.

Kama ilivyoandikwa...nabii

Misitari 4-6 ni nukuu kutoka Isaya. Ingeweza kuelezewa katika hali ya kutenda. AT: "Hii ilitokea kama Isaya alivyokuwa ameandika katika kitabu chake" au "Yohana aliyatimiza maneno ambayo Isaya alikuwa ameyaandika katika kitabu chake."

Sauti ya mtu inapazwa nyikani

Hii inaweza kudhihirishwa kama sentensi. NI: "Sauti ya mmoja inapazwa ikisikika katika nyika" au "Wanasikia sauti ya mtu fulani inapazwa katika nyika"

Itengenezeni njia ya Bwana ... tengeneza mapito kwa unyoofu

Kauli hizi mbili kimsingi ni kitu kile kile.

Tayarisha njia ya Bwana

"Andaa njia kwaajili ya Bwana." Kufanya hivi kunawakilisha kujiandaa kusikia ujumbe wa Bwana anapokuja. Watu hufanya hivi kwa kutubu dhambi zao. NI: "Andaa kusikia ujumbe wa Bwana anapokuja" au "Tubu na uwe tayari kwaajili ya ujio wa Bwana"

njia

"pa kupita" au "barabara"

Luke 3:5

Kila bonde litajazwa...kila mlima na kilima vitasawazishwa

Watu wanapoandaa barabara kwa ajili ya mtu mhimu anayekuja, wanasawazisha maeneo yaliyoinuka na kujaza maeneo ya mabonde ili kusawazisha barabara. Hii ni sehemu ya msemo wa neno lililozungumzwa katika msitari ulioelezwa juu.

Kila bonde litajazwa

Hii inaweza kuelezewa katika hali ya kutenda. AT: "Watalijaza kila eneo la bonde katika barabara.

Kila mlima na kijilima vitasawazishwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. AT: "watasawazisha kila mlima na kilima"" au "Wataondoa kila eneo la mwinuko katika barabara"

Angalia wokovu wa Mungu

Hii inaweza kuelezewa kama tendo. AT: "Jifunze jinsi Mungu anavyookoa watu kutoka katika dhambi."

Luke 3:7

Kubatizwa na Yeye

Hii inaweza kuelezewa katika hali ya kutenda. AT: "Kwa Yohana kuwabatiza"

Enyi kizazi cha Nyoka wenye sumu

Katika sitiari hii, nyoka wenye sumu ni hatari na wanawakilisha uovu. AT: "Ninyi nyoka waovu wenye sumu!" au "Ninyi ni waovu kama nyoka wenye sumu."

Nani aliyewaonya ... kuja?

Hakuwatarajia haswa kujibu. Yohana alikuwa anawakemea watu kwasababu walikuwa wanamwomba awabatize, lakini hawakutaka kuacha kutenda dhambi. AT: "Hamwezi kuikimbia gadhabu ya Mungu namna hii" au "Hamwezi kuepuka gadhabu ya Mungu kwa kubatizwa."

Kutoka kwenye ghadhabu inayokuja

Neno "gadhabu" linatumika hapa kumaanisha adhabu ya Mungu kwa sababu gadhabu yake inaizidi hiyo. AT: "kutoka kwenye adhabu ambayo Mungu anaituma" au "kutoka kwenye gadhabu ya Mungu ambayo yuko karibu kuiachilia"

Luke 3:8

Zaeni matunda yanayoendana na toba

Katika mfano huu, tabia ya mtu inalinganishwa na mti. Kama tu kwa mmea linavyotarajiwa kuzaa tunda linaloendana na aina ya mmea, mtu ambaye anasema kwamba ametubu, anatarajiwa kuishi kwa haki. AT: "Zaeni aina ya tunda linaloonyesha kwamba umetubu" au "fanya mambo mema yanayoonyesha kwamba umegeuka kutoka katika dhambi zako."

Mkisema wenyewe ndani yenu

"Kusema mwenyewe" au "kufikiri mwenyewe"

Tuna Ibrahimu aliye baba yetu

"Abrahamu ni Baba yetu" au Sisi ni uzao wa Ibrahimu. "kama inaeleweka kwanini wangesema hili, unaweza pia kuongeza habari imaanishayo: "Hivyo Mungu hatatuadhibu sisi."

Kumwinulia Ibrahimu watoto

Nahau hii inamaanisha "Umba watoto kwa ajili ya Ibrahimu" au "sababisha watu kuwa wafuasi wa Ibrahimu."

Kutokana na mawe haya

Labda Yohana alikuwa anamaanisha mawe halisi kando ya Mto Yordani.

Luke 3:9

Shoka limeshawekwa dhidi ya mzizi wa miti

Shoka ambalo liko tayari kukata mizizi ya mti ni mfano wa adhabu iliyo karibu kuanza. Inaweza pia kuelezwa katika hali ya kutenda. AT: "Mungu ni kama mtu aliyeweka shoka lake dhidi ya mzizi wa miti."

Kila mti usiozaa tunda jema hukatwa chini

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. AT: "Hukata chini kila mti usiozaa tunda jema."

Kutupwa motoni

"Moto" pia ni mfano wa adhabu. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. AT: "Hulitupa ndani ya moto"

Luke 3:10

Maelezo unganishi:

Yohana anaanza kujibu maswali ambayo watu kwenye mkutano wanamuuliza.

Walimuuliza, wakisema

"Walimuuliza na kusema" au Walimuuliza Yohana"

Alijibu na kusema kwao

"Aliwajibu, akisema" au "aliwajibu" au "alisema"

Fanya hivyohivyo

"Fanya jambo hilohilo." Inaweza kwa msaada kuelezea hasa inavyomaanisha. AT: "Mpe chakula mtu ambaye hana kabisa."

Luke 3:12

Kubatiza

Hii ingeweza kuelezwa katika hali ya kutenda. AT: "Kwa Yohana kuwabatiza."

Msikusanye fedha zaidi

"Msiombe fedha zaidi" au "Msitake fedha zaidi." Watoza ushuru walikuwa wakikusanya fedha zaidi kuliko walivyokuwa wanatakiwa. Wanapaswa kuacha kufanya hivyo.

Zaidi kuliko mnavyotakiwa

Kifungu hiki kinaonyesha kwamba mamlaka ya watoza ushuru hutoka Rumi. AT: "zaidi kuliko kile Warumi wamewaamuru kuchukua."

Luke 3:14

Maaskari

"Watu wanaotumika jeshini"

Na sisi je? Tunapaswa kufanya nini?

Vipi na sisi maaskari, tunapaswa kufanya nini?" Yohana haunganishwi katika maneno "sisi" na "sisi." Maskari walimaanisha kwamba alikuwa amewaambia makutano na watoza ushuru wanachotakiwa kufanya na walitaka kujua kama maaskari wanachotakiwa kufanya.

Msimshutumu yeyote kwa uongo

Inaonekana kwamba maaskari walikuwa wanatengeneza tuhuma za uongo dhidi ya watu ili kujipatia fedha. AT: "kwa namna ileile, msimshutumu yeyote kwa uongo ili mjipatie fedha kutoka kwao" au "Msiseme kwamba mtu asiye na hatia amefanya kitu kinyume cha sheria."

Rizikeni na mishahara yenu

"Toshekeni na malipo yenu"

Luke 3:15

Kama watu

"Kwa sababu watu." Hii inamaanisha watu walewale waliokuja kwa Yohana.

wasiwasi katika mioyo yao

Udhihirisho huu hapa unamaanisha "fikiria juu yao kwa utulivu"

Yohana alijibu kwa kusema

Jibu la Yohana kuhusiana na mtu mkuu ajaye ni wazi inamaanisha Yohana siyo Kristo. Inaweza kusaidia kusema hili wazi kwaajili watu wako, kama UDB, inavyofanya. "Hapana, Mimi siye"

Nawabatiza kwa maji

"Nawabatiza kwa kutumia maji" au "Nawabatiza kwa nyenzo ya maji"

Haistahili hata kufungua kamba za viatu vyake

Kufungua kamba za viatu ilikuwa ni wajibu wa mtumwa. Yohana alikuwa anasema kwamba yule atakayekuja ni mkubwa kiasi kwamba Yohana hakustahili hata kuwa mtumwa wake. AT: "Hafikii umuhimu hata kulegeza kamba za viatu vyake."

Viatu

"Viatu vilivyotengenezwa kwa ngozi" au "Aina ya viatu vya wazi vyenye kamba za ngozi"

Atawabatizeni kwa Roho Mtakatifu na kwa moto

Huu mfano unalinganisha ubatizo wa kawaida unamleta mtu katika muunganiko na maji kwenye ubatizo wa kiroho unaowaleta katika muunganiko na Roho Mtakatifu na moto.

Moto

Hapa neno "moto" linamaanisha 1) hukumu au 2) utakaso. Inafaa kuionda kama moto

Luke 3:17

Pepeteo lake liko mkononi mwake

Kama mkulima alivyo tayari kutenganisha mbegu za ngano kutoka kwenye pumba hivyo, ndivyo ilivyo kwa Kristo alivyo tayari kumhukumu mwanadamu. AT: "Anashikilia pepeteo kwasababu yuko tayari."

Pepeteo

Hiki ni chombo cha kurushia ngano juu hewani kutenganisha mbegu kutoka kwenye pumba. Mbegu nzito huanguka kurudi chini na pumba azisizotakiwa hupulizwa mbali na upepo. Inafanana na kirushio.

Uwanda wake wa kupepetea

Mahali pa kupepetea ni eneo ambapo ngano iliwekwa katika kuiandaa kuipepeta. "Kusafisha" AT: "Eneo lake" au "Eneo ambako hutenganisha mbegu kutoka kwenye pumba"

Kukusanya ngano

Ngano ni nafaka inayokubalika kuitunza na kuhifadhi.

Kuzichoma pumba

Pumba hazitumiwi kwa chochote, hivyo, watu huyachoma zote.

Luke 3:18

Maelezo kwa ujumla

Simulizi inaelezea nini kinaenda kutokea kwa Yohana lakini halijatokea kwa wakati huu.

Kwa maonyo mengine mengi

"Pamoja na hoja zingine za nguvu nyingi"

Herode Tetraki

Herode alikuwa Tetraki, siyo mfalme. Alikuwa na utawala unaokomea eneo maalumu katika mkoa wa Galilaya.

Kwaajili ya kumuoa mke wa ndugu yake Herodia

"kwa sababu Herode alimuoa Herodia, mke wa ndugu yake." Huu ulikuwa uovu kwa sababu kaka wa Herode alikuwa hai. Hii inaweza kusemwa wazi. AT: "kwasababu alimuoa mke wa kaka yake, Herodia, wakati kaka yake akiwa hai"

Alimfunga Yohana gerezani

"Aliwaambia askari wake kumuweka Yohana jela

Luke 3:21

Sentensi unganishi

Yesu anaanza huduma yake kwa ubatizo wake.

Sasa ikawa kwamba

Msemo huu ni mwanzo wa tukio jipya katika hadithi. Kama lugha yako ina njia kwa ajili ya kufanya hii, unaweza kufikiria kutumia hapa.

wakati watu wote walikuwa wakibatizwa na Yohana

"Wakati Yohana alikuwa akibatiza watu wote." Neno "watu wote" inahusu watu akiwemo na Yohana.

batizwa

"Yesu alibatizwa na Yohana." Baadhi ya makundi wanaweza kuchanganywa kwamba Yohana alikuwa anabatiza wakati Herode alimweka gerezani kwenye mstari uliotangulia. Ikiwa hivyo, inaweza ikasaidia kuwaambia kwamba tukio hili lilitokea kabla Yohana hajakamatwa. UDB inaliweka hivi "Lakini kabla ya Yohana hafungwa gerezani" mwanzoni mwa mstari huu.

Yesu pia alibatizwa

Hii inaweza kusemwa katika mfumo wa kutendea. NI: "Yohana alimbatiza Yesu, vilevile"

mbingu zimefunguka

"Anga likafunguliwa" au "anga likawa wazi." Hii ni zaidi ya kusafisha mawingu, lakini siyo wazi nini maana yake. Ni uwezekano ina maana kwamba shimo alionekana katika anga.

Roho Mtakatifu kwenye umbo la mwili alishuka juu yake

"Roho Mtakatifu akashuka juu Yesu"

kama la njiwa

"Katika hali ya kimwili Roho Mtakatifu alionekana kama njiwa"

Wewe ni Mwanangu, ambaye nakupenda

Mungu Baba anaongea na Mwanaye ("ambaye nampenda"), Yesu ni Mungu Mwana, wakati Mungu Roho shuka juu ya Yesu. watu wa Mungu kupendana na kufanya kazi pamoja kama Baba, Mwana, na Roho.

Mwanangu, ambaye nampenda

Hili ni jina muhimu kwa Yesu, Mwana wa Mungu

Luke 3:23

Maelezo kwa ujumla

Luka anaorodhesha mababu wa Yesu kwa njia ya uzao wa baba yake mlezi, Yusufu.

Wakati

Neno hili limetumika hapa kuthibitisha mabadiliko kutokana na hadithi ya taarifa za msingi kuhusu kuhusu umri Yesu na mababu.

umri wa miaka thelathini

"umri wa miaka 30"

Alikuwa mwana (kama ilivyodhaniwa) wa Yusufu

"Ilidhaniwa kwamba alikuwa ni mwana wa Yusufu" au "Watu walidhani kuwa yeye ni mwana wa Yusufu"

mwana wa Eli, mwana wa Mathati, mwana wa Lawi

fikiria jinsi watu wanavyoorodhesha wahenga katika lugha yako. Utumie mfumo huohuo kwa orodha yote. Mifumo inyoowezekana ni 1) "ambaye alikuwa mwana wa Heli, ambaye alikuwa mwana wa Mathat, ambaye alikuwa mwana wa Lawi" 2) Yusufu alikuwa mwana wa Heli, Heli alikuwa mwana wa Mathat, baba wa Mathat alikuwa Lawi"

mwana wa Eli.

"Yusufu alikuwa mwana wa Eli" au "baba Yusufu alikuwa Eli"

Luke 3:25

mwana wa Matathia, mwana wa Amosi ... Joda

Huu ni mwendelezo wa orodha ya mababu wa Yesu. Tumia namna ile ile kama ulivyotumia kwenye mistari ile iliyotangulia.

Luke 3:27

mwana wa Yohanani, mwana wa Resa ... Levi

Matumizi maneno sawa kama wewe kutumika katika mistari uliopita. AT "ambaye alikuwa mwana wa Yohanani, ambaye alikuwa mwana wa Resa ... Levi" au "Joda alikuwa mwana wa Yohanani, Yohanani mwana wa Resa ... Levi" au "baba Joda ilikuwa Yohanani, baba Yohanani aliitwa Rhesa ... Levi. " Hii ni muendelezo wa orodha ya mababu Yesu.

Luke 3:30

mwana wa Simoni, mwana wa Yuda

Matumizi maneno sawa kama wewe kutumika katika mistari uliopita. "Ambaye alikuwa mwana wa Simeoni ambaye alikuwa mwana wa Yuda" au "Levi mwana wa Simeoni, Simeoni alikuwa mwana wa Yuda" au" baba Levi aliitwa Simeoni, baba Simeon alikuwa Yuda"

Luke 3:33

mwana wa Aminadabu, mwana wa Admini

Matumizi maneno sawa kama wewe ulivyotumika katika mistari iliyopita. "Ambaye alikuwa mwana wa Aminadabu, ambaye alikuwa mwana wa Admini" au "Levi alikuwa mwana wa Aminadabu, Simeoni ni mwana wa Admini" au "baba Nashon ilikuwa Aminadabu, Aminadabu baba aliitwa Admin"

Luke 3:36

mwana wa Kainani, mwana wa Arfaksadi

Tumia maneno sawa kama uliyotumia katika mistari iliopita. "Ambaye alikuwa mwana wa Kenani, ambaye alikuwa mwana wa Arfaksadi" au "Levi alikuwa mwana wa Kenani, Kenani alikuwa mwana wa Arfaksadi" au "baba Shela alikuwa Kenani, Kenani baba aliitwa Arfaksadi"

Luke 4

Luka 04 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri hupendelea kuweka mbele kidogo nukuu za Agano la Kale. ULB na tafsiri nyingine nyingi za Kiingereza huingiza mistari ya 4:10-11, 18-19, ambayo ni nukuu kutoka Agano la Kale.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Yesu alijaribiwa na shetani

Ingawa ni kweli kwamba shetani aliamini kwa hakika kwamba angeweza kumshawishi Yesu kumtii, ni muhimu kuonyesha kama Yesu hakutaka kumtii hata kidogo.

<< | >>

Luke 4:1

Sentensi Unganishi

Ibilisi amkuta Yesu aweze kumjaribu akose baada ya Yesu kufunga kwa siku arobaini 40.

Ndipo Yesu

Hii inarejea baada ya Yohana kumbatiza Yesu. NI: "Baada ya Yesu kuwa kabatizwa"

akaongozwa na Roho

Hii inaweza katika mfumo wa kutenda. NI: "Roho alimwongoza"

Kwa siku arobaini yeye alijaribiwa

Tafsiri nyingi zinasema kwamba majaribu yalikuwa kwa siku zote arobaini. UDB inasema "Wakati akiwa pale, Ibilisi aliendelea kumjaribu" kuweka hili wazi.

siku arobaini

"siku 40"

alikuwa akijaribiwa na shetani

Hii inaweza kusemwa katika mfumo wa kutenda. NI: "ibilisi alimjaribu asimtii Mungu"

Hakuna alichokula

Neno "yeye" linarejea kwa Yesu.

Luke 4:3

Kama ni mwana wa Mungu

Ibilisi anamtega Yesu afanye muujiza huu ili kwamba athibitishe yeye ni "mwana wa Mungu"

hili jiwe

Ibilisi ama anashikilia jiwe au ananyooshea kidole kwenye jiwe lililokaribu.

Yesu alimjibu

Kukataa kwa Yesu kukosolewa na Ibilisi iko wazi kwenye jibu lake. Itaweza kusaidia kusemwa hili kwa wazi kwa kundi lako, kama inavyofanya UDB "Yesu alijibu, Hapana, sitafanya hivyo"

Hii imeandikwa

Nukuu inatoka kwa Maandiko ya Musa katika Agano la Kale. Hii inaweza kusemwa kwa kauli tendaji. NI: "Musa ameandika katika maandiko"

Mtu haishi kwa mkate pekee

Neno "mkate" linarejea kwenye chakula kwa ujumla. Chakula kama ukilinganisha kwa Mungu, chenyewe tu, hakitoshi, kumtosheleza mtu. Yesu ananukuu maandiko kwanini asibadili jiwe mkate. NI: "watu hawahawezi kuishi kwa mkate tu" au "siyo chakula tu ambacho kinamfanya mtu aishi" au "Mungu anasema vitu mhimu zaidi ya chakula"

Luke 4:5

mahali pa juu

mlima mrefu

katika muda mfupi

hapo hapo au "kwa ghafla"

nimepewa mimi haya

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. Huenda kwamba maana "wao" inarejea 1) mamlaka na fahari ya falme au 2) falme NI: "Mungu ameyatoa kwangu"

kama utainama chini ... kuniabudu

Kauli hizi mbili zinafanana sana. Zinaweza kuwekwa pamoja. NI: "kama utainama chini katika kuniabudu"

Itakuwa ya kwako

"Nitakupa wewe ufalme hizi zote, pamoja na fahari zake"

Luke 4:8

Lakini Yesu alijibu ... imeandikwa

Utofauti huu unamaanisha kwamba Yesu alikataa kufanya kile alichoambiwa na Ibilisi. Itakuwa msaada kusema hiki wazi kwa hadhara yako. NI: "Lakini alijibu, 'Hapana, sitakuabudu wewe, kwa sababu imeandikwa" (UDB)

alijibu na akamwabia

"akamjibu" au "alimjibu"

Imeandikwa

Hii inaweza ikasemwa katika kauli tendaji. NI: "Musa ameandika katika maandiko"

Utamwabudu Bwana Mungu wako

Yesu alikuwa ananukuu amri kutoka kwenye maandiko kusema kwanini hataweza kumwabudu Ibilisi.

Wewe

Hii inarejea kwa watu katika Agano la Kale waliopokea amri ya Mungu. Unawea kutumia kauli ya umoja 'wewe' sababu kila mtu ilikuwa atiii, au ungetumia kauli ya wingi "ninyi" sababu watu walipaswa kuitii.

yeye

Neno "yeye" anarejea kwa Mungu.

Luke 4:9

ncha ya juu sana

Hii ilikuwa ni ncha kwenye paa la hekalu. Kama mtu akianguka kutokea kule, angejeruhiwa sana au kufa.

Kama wewe ni mwana wa Mungu

shetani alikuwa anamkosoa Yesu athibitishe kwamba alikuwa Mwana wa Mungu

Mwna wa Mungu

Hiki ni cheo mhimu kwaajili ya Yesu.

jitupe mwenyewe chini

"ruka chini ardhini"

Kwa kuwa imeandikwa

Ibilisi anamaanisha kwamba nukuu yake kutoka Zaburi inamaanisha Yesu hataumia kama ni Mwana wa Mungu. Hii inwaeza kusemwa wazi, kama inavyofanya UDB. NI: "Hutaumia" sababu imeandikwa"

imeandikwa

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. NI: "mwandishi ameandika"

Yeye atatoa maagizo

"Yeye" inarejea kwa Mungu. Ibilisi kwa sehemu alinukuu kutoka Zaburi kwa juhudi kumshawishi Yesu kuruka kutoka juu ya jengo.

Luke 4:12

Hii ilisemwa

Yesu anamwambia Ibilisi kwanini hatafanya kile ambacho Ibilisi amemwabia kufanya. Kukataa kwake kufanya inaweza kusemwa wazi. NI: "Hapana, sitafanya hivyo, kwasababu ilisemwa"

Hii ilisemwa

Yesu ananukuu kutoka maandiko ya Musa katika Kumbukumbu la Torati. Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. NI: "Musa amesema" au "katika maandiko Musa alisema"

Usimweke Mungu wako katika majaribu

Maana zinazowezekana ni 1) Yesu hataweza kumjaribu Mungu kwa kuruka kutoka katika hekalu, au 2) Ibilisi hawezi kumjaribu Yesu kuona kama yeye ni Mwana wa Mungu. inafaa zaidi kutafsiri mstari kama ilivyoelezwa zaidi kuliko kujaribu fafanua maana.

Mpaka wakati mwingine

"mpaka tukio lingine"

lishamaliza kumjaribu Yesu

Hii haimaanishi kwamba Ibilisi alikuwa kafanikiwa katika majaribu yake - Yesu alipinga kila jaribio. Hii inaweza ikasemwa wazi. Ni: "lishamaliza kujaribu kumjaribu Yesu" (UDB) au "pumzika kujaribu kumjaribu Yesu"

Luke 4:14

Sentensi Unganishi:

Yesu alirudi Galilaya, akifundisha katika Sinagogi, na anawaambia watu pale kwamba yeye anatimiza maandiko ya Isaya nabii.

Ndipo Yesu alirudi

Hii inaanza simulizi jipya katika habari.

katika nguvu ya Roho

"na Roho alikuwa anampa yeye nguvu." Mungu alikuwa pamoja na Yesu kwa namna maalumu, anamwezesha yeye kufanya vitu ambayo kawaida watu wasingeviweza.

habari kumhusu yeye zikaenea

Wale waliomsikia Yesu waliwaambia watu wengine kuhusu yeye, na ndipo wale watu wengine waliwaambia hata zaidi kuhusu yeye. Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. NI: "watu wakaeneza habari kuhusu Yesu" au "watu waliwaambia watu wengine kuhusu Yesu" au "maarifa kumhusu yeye yalikuwa yakipita kutoka kwa mtu kwenda mtu mwingine"

kupitia katika eneo lote linalozunguka ukanda

Hii inarejea kwenye maeneo au mahali karibu na Galilaya.

likuwa anasifiwa na wote

"kila mmoja alisema mambo makuu kuhusu yeye" au "watu wote walimsema vizuri "

Luke 4:16

mahali yeye alipokuziwa

mahali wazazi wake walipomlelea " au "pale alipoishi alipokuwa mdogo" "mahali alipokulia"

kama ilivyokuwa desturi yake

"kama alivyofanya kila sabato." ilikuwa siyo mazoea ya kawaida kwenda kwenye sinagogikwenye siku ya sabato.

Yeye alipewa Gombo la nabii Isaya

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. NI: "mtu fulani alimpa gombo la nabii Isaya"

Gombo la nabii Isaya

Hii inarejea kwenye kitabu cha Isaya imeandikwa kwenye gombo. Isaya aliandika maneno miaka mingi kabla, na mtu fulani mwingine aliyanukuru kwenye gombo.

mahali ambapo palikuwa pameandikwa

"mahali katika gombo palipo na maneno haya." Sentensi hii inaendelea katika mstari unaofuata.

Luke 4:18

Roho wa Bwana iko juu yangu

"Roho Mtakatifu yuko pamoja nami kwa namna maalumu." Wakati mtu fulani anasema hivi, anathibitisha kunena maneno ya Mungu.

aliniweka wakfu mimi

Katika Agano la Kale, mafuta ya upako yalimiminwa juu ya mtu aliyepewa nguvu na mamlaka kufanya kazi maalumu. Yesu anatumia sitiari hii kurejea kwa Roho Mtakatifu kuwa juu yake kumwandaa kwaajili ya kazi. NI: "Roho Mtakatifu yuko juu yangu kuniwezesha" au "Roho Mtakatifu alinipa mimi nguvu na mamlaka"

maskini

"watu maskini"

kutangaza uhuru kwa mateka

"kuwaambia ambao walikuwa wametekwa kwamba wako huru" au "kuwaweka huru wafungwa wa vita"

kupona macho kwa wale vipofu

"kumpa kipofu kuona" au "kumfanya kipofu aweze kuona tena"

wekwa huru wale ambao wanagangamizwa

"weka huru wale ambao tumikishwa vibaya"

kutangaza mwaka wafadhila ya Bwana

"mwambia kila mmoja kwamba Bwana tayari amebariki watu wake" au "tangaza kwamba huu ni mwaka ambao Bwana ataonesha wema wake"

Luke 4:20

bingilisha gombo

gombo lilikuwa limefungwa kwa kubingilishwa kama bomba kutunza kile kilichoandikwa ndani yake.

mhudumu

Hii inarejea kwa mtumishi wa sinagogi ambaye alileta na kutunza kwa uangalifu and unyenyekevu gombo linalobeba maandiko.

yalikuwa yamekazwa kwake

Lahaja hii inamaanisha "yalikuwa yameelekezwa kwake" au "walitazama kwa makini kwake"

maandiko haya yametimizwa mkiwa mnasikiliza

Yesu alikuwa anasema hivyo kutimiza unabii kwa vitendo na hotuba kwa wakati wake kabisa. Hii inaweza ikaelezwa katika kauli tendaji. NI: "Sasa hivi ninatimiza inatimiza ambacho maandiko yalisema mnaponisikiliza sasa"

shangazwa na maneno ya neema ambayo yalikuwa yanatoka katika kinywa chake

"lipigwa butwaa na vitu vya neema alivyokuwa akivisema." Hapa "aneema" inaweza kuerejea 1) ubora au jinsi ya ushawishi aliozungumza Yesu, au 2) kwamba Yesu alizungumza maneno kuhusu neema ya Mungu.

Huyu si ni mwana wa Yusufu?

Watu walifikiri kwamba Yusufu alikuwa baba wa Yesu. Yusufu hakuwa kiongozi wa dini, hivyo walishangaa kwamba mtoto wake atahubiri kiasi hicho. NI: "Huyu ni mwana wa Yusufu tu!" au "Baba yake ni Yusufu tu!"

Luke 4:23

Maelezo kwa Ujumla

Nazarethi ni mji ambao ndimo Yesu alikulia

Kwa hakika

"Kwa hakika" au "bila shaka." Huu ni uthibitisho wa nguvu.

Daktari, jiponye mwenyewe!

Kama daktari haonekani kuwa ana afya, hakuna sababu kumwamini kuwa kweli ni daktari. Wakati watu wanasema mithali hii kwa Yesu, watamaanisha hawakuamini kwamba yeye ni nabii sababu hafanani.

lolote tulilosikia ... fanya hivyo hivyo kwenye miji ya kwenu.

Watu wa Nazarethi hawakuamini Yesu kuwa nabii sababu ya sifa yake ya chini kama mtoto wa yusufu. Hawataamini isipokuwa waone wao wenyewe akifanya miujiza.

Ukweli nasema kwenu

"Hii kweli ni hakika." Hii ni kauli ya msisitizo kuhusu kile kinachofuata.

hakuna nabii anayepokelewa kwenye mji wa kwao

Yesu anaitengeneza kauli hii kwa ujulma ili kwmba awakemee watu. Yeye anamaanisha kwamba wanakataa kuamini taarifa za miujiza yake Kapernaumu. Wao walifikiri tayari walijua yote yanayomhusu yeye.

mji wa kwao

"ardhi yao" au "wenyeji wa mji" au "nchi ambayo alikulia"

Luke 4:25

Sentensi kwa Ujumla

Yesu anawakumbusha watu, wanaomsikiliza kwenye sinagogi, kuhusu Eliya na Elisha waliokuwa manabii ambao waliwafahamu.

Lakini nawaambia ukweli

"Nawaambia ukweli kabisa." Kauli hii ilitumika kusisitiza umhimu, ukweli na usahihi wa kauli zinazofuata.

wajane

mjane ni mwanamke aliyefiwa na mume wake.

wakati wa Eliya

Watu wale aliokuwa anawahutubia walijua kwamba Eliya alikuwa mmoja wa manabii wa Mungu. Kama wasomaji wako hawatajua hilo, unaweza ukafanya taarifa zisizowazi kuwa wazi kma UDB. AT: "Eliya alipokuwa anatoa unabii Israel"

wakati wingu lilipofungwa

Hii ni sitiari. Anga limefananishwa na dari iliyofungwa, na hivyo hakuna mvua itakayonyysha toka huko. NI: "ambapo hakuna mvua inashuka chini kutoka angani" au "wakati ilikuwa hakuna mvua kabisa"

njaa kubwa

"tatizo kubwa la kupungua chakula." Njaa ni kipindi kirefu ambapo hakuna uzalishaji wa mazo ya kutosha chakula kwa watu.

mpaka Sarepta ... kwa mjane anayeishi huko

Watu walioishi Sarepta walikuwa Wamataifa, siyo Wayahudi. Watu wanaomsikiliza Yesu wangeelewa kwamaba watu wa Sarepta walikuwa Wamataifa. Mjane mmataifa anaishi Sarepta.

Naamani Msiria

Msiria ni mtu kutoka nchi ya Siria. Watu wa Siria ni siyo Wayahudi. NI: "Mmataifa Naamani kutoka Siria"

Luke 4:28

Watu wote kwenye sinagogi walijaa hasira waliposikia mambo haya

Watu wa Nazarethi walikosewa sana kwamba Yesu alidondoa maandiko ambayo Mungu aliwasaidia wamataifa badala ya Wayahudi.

walimlazimisha yeye atoke nje ya mji

"walimlazimisha yeye kuuacha mji" au "alisukumwa nje ya mji" (UDB)

jabali la kilimani

"ncha ya jabali"

yeye alipitia katikati yao

"kupita katikati ya mkutano" au "kati ya watu ambao wanajaribu kumuua yeye." Neno "haki" hapa ni sawa na neno "rahisi." Linaashiria kwamba hakuna kilichomzuia yeye kuweza kutembea kupitia mkutano wenye hasira.

alikwenda sehemu nyingine

"alikwenda mbali" au "alikwenda kwa njia yake" Yesu alikwenda ambako alikuwa kapanga kwenda badala ya ambako watu walijaribu kumlazimisha aende.

Luke 4:31

Sentensi Unganishi

Yesu anakwenda Kapernaumu, anafundisha watu katika Sinagogi huko, na anaamuru mapepo kuondoka kwa mtu.

Ndipo yeye

"ndipo Yesu." Hii inaashiria tukio jipya.

alishuka Kapernaumu

Kirai hiki "shuka chini" ilitumika hapa sababu Kapernaumu ni chini kuliko Nazarethi.

Kapernaumu, ni mji katiaka Galilaya

"Kapernaumu, mji mwingine katika Galilaya"

liostaajabisha

"lishangaa sana" au "liovutia sana" au "lioshangaza "

alizungumza kwa mamlaka

"alizungumza kama mtu mwenye mamlaka" au "maneno yake yalikuwa na nguvu kubwa"

Luke 4:33

Sasa ... alikuwepo mtu

Kirai hiki kinatumika kudokeza utangulizi wa mhusika mpya ndani ya simulizi; katika suala hili, mtu aliyepagawa pepo.

ambaye alikuwa na pepo mchafu

"ambaye alipagawa na pepo mchafu" au "ambaye alitawaliwa na na roho mchafu" (UDB)

alilia kwasauti ya juu

"yeye alipiga kelele"

Tunanini cha kufanya na wewe

Hili jibu la kichokozi ni nahau ambayo inamaana: "Nini tulichonacho cha kufanana?" au "unahaki gani ya kutusumbua sisi?"

Nini cha kufanya na wewe, Yesu wa Nazarethi?

Swali hili lingeandikwa kama sentensi. NI: "Nini wewe, Yesu wa Nazarethi, unataka kutufanyia" au Hakuna chochote cha kufanya na wewe, Yesu wa nazarethi!" au "Huna haki kutusumbua sisi, Yesu wa Nazarethi!"

Luke 4:35

Yesu alikemea pepo, akisema

"Yesu alikemea pepo akisema," au "Yesu bila huruma alisema kwa pepo"

toka nje yake

Yeye alimwamuru pepo kutokumtawala mtu. NI: "mwache peke yake" au "usiishi ndani ya mtu huyu tena"

Haya ni maneno ya aina gani?

Watu wanadhihirisha jinsi walivyoshangazwa kwamba Yesu anamamlaka kuamuru pepo kumwacha mtu. Hii inaweza kuandikwa kama sentensi. NI: "Haya maneno yanashangaza!" au "maneno yake ya ajabu"

Anaamuru roho wachafu kwa mamlaka na nguvu

"Yeye anamamlaka na nguvu kuamuru roho wachafu"

Habari kumhusu zilianza kuenea ... kanda inayozunguka

Hii ni amri kuhusu kile kilichotokea baada ya simulizi ambacho kilisababishwa na matukio ndani ya hadithi yenyewe.

habari kumhusu yeye zilianza kuenea

"taarifa kuhusu Yesu zilianza kuenea" au "watu walianza kueneza habari kuhusu Yesu"

Luke 4:38

Sentensi Unganishi

Yesu bado yuko Kapernaumu, lakini sasa yuko katika nyumba ya Simoni, alipomponya mama mkwe wa Simoni na watu wengi.

Ndipo Yesu akaondoka

Hii inaanzisha tukio jipya

Mama mkwe wa Simoni

Mkwe - "mama yake mke wa Simoni"

Alikuwa anaumwa

Hii ni nahau inayomaanisha "alikuwa anaugua"

homa kali

"mwili wake ulikuwa na joto kali"

kusihi badala yake

Maana yake walimwomba Yesu amponye homa yake. Hii inaweza kusemwa wazi. NI: "kumwomba Yesu amponye homa"

Hivyo alisimama

Neno "Hivyo" linaweka wazi kwamba alifanya hivi kwa sababu watu walimsihi badala ya mama mkwe wa Simoni.

alisimama kwake

"alikwenda kwake na aliegama kwake"

liikemea homa

"alisema kwa kuikaripia homa" au "aliamuru homa kumwacha" UDB. Itakuwa ni msaada kusema wazi alichoiambia homa kufanya. NI: "aliiamuru ngozi kupoa" "aliuamuru ugonjwa kumwacha"

alianza kuwahudumia

Hapa hii inamaana alianza kuandaa chakula kwaajili ya Yesu na watu wengine ndani ya nyumba.

Luke 4:40

alilaza mkono wake juu

"aliweka mkono wake juu" au "aligusa"

Pepo pia yakatoka nje

Hii ilimaanisha kwamba Yesu aliyafanya mapepo yaondoke kwa watu yaliokuwa yamewatawala. Hii inaweza kusemwa wazi. NI: "Yesu pia aliyalazimisha mapepo yatoke"

analia kwa sauti na akisema

inamaanisha kitu kilekile, na huenda inarejea kulia kwa hofu au hasira. Baadhi ya tafsiri inatumia neno moja. NI: "paza sauti"

Mwana wa Mungu

Hiki ni cheo mhimu kwa Yesu.

alikemea pepo

"aliwaambia pepo kwa ukali"

usingeliwaruhusu

"Wao hapana kuwaruhusu"

Luke 4:42

Sentensi Unganishi:

Ingawa watu walitaka Yesu abaki Kapernaumu, anakwenda kuhubiri kwenye masinagogi mengine Uyahudi.

ilipofika mapambazuko

"wakati wa jua kuchomoza"

mahali palipo jitenga

"mahali pa pekee" au "mahali pasipokuwa na watu"

kwa miji mingi mingine

"kwa watu katika miji mingine mingi"

hii ni sababu nilikuwa nimetumwa hapa

Hii inaweza ikawekwa kwenye kauli tendaji, NI: "hii ni sababu Mungu alinituma hapa mimi"

Uyahudi

Tangu Yesu awe Galilaya, neno "Uyahudi" hapa huenda linarejea kwenye ukanda wote ambako Wayahudi waliishi wakati huo, NI: "ambapo waliishi Wayahudi"

Luke 5

Luka 05 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

"Utavua watu"

Agano Jipya mara nyingi huzungumzia juu ya kufanya wanafunzi au wafuasi wa Kristo. Hii ni huduma kuu ya kanisa. Kuna takwimu nyingi tofauti zinazotumiwa kuelezea hii katika Agano Jipya. Katika sura hii, Yesu anatumia mfano wa uvuvi kueleza kuwa wanafunzi wa Kristo wanapaswa kukusanyika watu wengine wawe wanafunzi wa Kristo. Yesu anamsaidia mvuvi Simoni kuvua samaki wengi sana ili kuonyesha kwamba Yesu atawawezesha Simoni na wanafunzi wengine kukusanyika wau wengi kumfuata Kristo. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#disciple and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

"Watu wenye dhambi"

Mafarisayo hutaja kundi la watu kuwa "wenye dhambi." Walikuwa wanamaanisha ni watu ambao hawakuwa na nia ya kufuata Sheria ya Musa. Hata hivyo, Luka anatumia neno "wenye dhambi" kama maneno ya kuzihaka, kwa sababu Yesu anasema kwamba alikuja kuwaita wenye dhambi kutubu. Kwa kutaja "wenye dhambi," Yesu alikuwa akimaanisha mtu yeyote mwenye hatia ya dhambi. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-irony)

Kufunga na Karamu

Kufunga mara nyingi kulifanyika wakati wa toba. Hakukufanyika wakati wa furaha. Kwa kuwa wakati ambapo Yesu alikuwa pamoja na wanafunzi wake ilikuwa wakati wa furaha, aliwaambia kama watafunga kwa wakati hayuko pamoja na wao tena. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#repent)

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Hali ya Kufikiri

Yesu anatumia hali ya kufikiri kuwahukumu Mafarisayo. Kifungu hiki kinajumuisha "watu wenye afya njema" na "watu wenye haki." Hii haimaanishi kwamba kuna watu ambao hawahitaji Yesu. Hakuna "watu wenye haki," kila mtu anahitaji Yesu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-hypo and Luke 5:31-32)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Maelezo yaliyodokezwa

Katika sehemu kadhaa za sura hii mwandishi alidokezea habari fulani ambayo wasomaji wake wa awali wangeelewa na kuwazia. Wasomaji wa kisasa labda hawajui mambo hayo yote, hivyo wanaweza kuwa na shida kuelewa mambo yote yaliyoandikwa na mwandishi. UDB mara nyingi huonyesha jinsi habari hiyo inaweza kutolewa ili wasomaji wa kisasa waweze kuelewa vifungu hivi. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-unknown and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

Matukio ya zamani

Sehemu za sura hii ni mfululizo wa matukio ambayo tayari yametokea. Katika kifungu fulani, wakati mwingine Luka anaandika kana kwamba matukio yamekwisha kutokea wakati matukio mengine bado yanaendelea (ingawa yamekamilika wakati anaandika). Hii inaweza kusababisha shida katika kutafsiri kwa kuunda utaratibu wa matukio usiofaa. Inaweza kuwa muhimu kufanya haya thabiti kwa kuandika kana kwamba matukio yote yamekwisha kutokea.

"Mwana wa Binadamu"

Yesu anajiita mwenyewe kama "Mwana wa Binadamu." Lugha zingine haziwezi kuruhusu mtu kujitaja mwenyewe kama 'mtu wa tatu.' (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sonofman)

<< | >>

Luke 5:1

Kauli Unganishi:

Yesu anahubiri kutoka katika mtumbwi wa Simoni Petro katika ziwa Genesareti

Sasa ilitokea

Kauli hii inatumika hapa kuweka alama kwenye mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi. Kama lugha yako inanamna ya kufanya hivi, ungefikiri kutumia hapa.

ziwa Genesareti

Hili ni jina lingine la ziwa Galilaya. Galilaya ulikuwa upande magharibi wa ziwa, na na nchi ya Genesareti ulikuwa upande wa mashariki, hivyo ulikuwa unaitwa kwa majina yote.

kuosha nyavu zao

Walikuwa wanasafisha nyavu za kuvuvia ili wazitumia tena kupata samaki.

mitumbwi mmoja ambao ulikuwa wa Simoni

"mtumbwi unaomilikiwa na simoni"

akamwambia kuweka kwenye maji mbali kidogo kutoka kwenye ardhi

"alimwambia Petro kuusukuma mtumbwi zaidi kutoka ufuoni"

aliketi na akawafundisha watu

kuketi ilikuwa ni mfumo wa kawaida kwa mwalimu.

aliwafundisha watu tokea kwenye mtumbwi

"aliwafundisha watu akiwa amekaa kwenye mtumbwi." Yesu alikuwa katika mtumbwi mbali kidogo kutoka ufuoni na alikuwa anaongea na watu ambao walikuwa kwenye ufuo.

Luke 5:4

Alipokwisha kumaliza kuzungumza

"Yesu alipomaliza kuwafundisha watu"

ya maneno yako

"kwa sababu ya maneno yako" au "kwa sababu umeniambia kufanya hivi"

walipunga

walikuwa mbali sana kutoka ufuoni hivyo walifanya ishara, huenda kupunga mikono.

walianza kuzama

"mtumbwi ulianza kuzama." "mtumbwi ulianza kuzama kwa sababu samaki walikuwa wazito sana."

Luke 5:8

alianguka chini magotini pa Yesu

Maana zinazowezekana ni 1) "kuinama chini magotini pa Yesu" au 2) kulala chini miguuni ya ardhi miguuni pa Yesu" 3) "kupiga magoti mbele ya Yesu." Yesu hakuanguka kwa bahati mbaya. Yeye alifanya hivi kama ishara ya unyenyekevu na heshima kwa Yesu.

mtu mwenye dhambi

Neno hapa kwa "mtu" linamaanisha "mtu mzima mwanaume" na kwa ujumla zaidi "binadamu."

kamata samaki

"idadi kubwa ya samaki"

washirika pamoja na Simoni

"Wadau wa Simoni katika biashara ya uvuvi"

utakamata watu

Sura ya kukamata samaki imekuwa ikitumika kama sitiari kwa kukusanya watu kumfuata Kristo. NI: "utavua watu" au "mtakusanya watu kwaajili yangu" au "mtaleta watu kuwa wanafunzi"

Luke 5:12

Sentensi Unganishi

Yesu anamponya mkoma katika mji tofauti ambao hautajwi jina.

Ikawa

Kauli hii inaonesha tukio jipya katika simulizi.

mtu aliyejaa ukoma

"mtu alikuwa anaukoma." Hii inatambulisha mhusika mpya kwenye simulizi.

akaangukia kichwa

"alipiga magoti na kichwa kikagusa chini" au "aliinama mpaka chini" (UDB)

kama uko tayari

"kama unataka"

unaweza ukanifanya msafi

ilifahamika kwamba yeye alikuwa anamuuliza Yesu aponywe. Hii inaweza ikasemwa wazi. NI: tafadhali nisafishe, sababu unaweza

nifanye msafi ... uwe safi

Hii inarejea kwenye usafi wa ibada, lakini ilifahamika kwamba yeye si msafi kwasababu ya ukoma. Yeye hasa anamuuliza Yesu amponye maradhi yake. Hii inaweza kusemwa wazi. NI: "niponye ukoma hivyo nitakuwa msafi ... upone"

ukoma ukamwacha

"hakuwa naukoma tena" (UDB)

Luke 5:14

kutomwambia mtu

Hii tafsiri inaweza ikanukuiwa moja kwa moja. "kutomwambia mtu kwamba wewe umeponywa." Ni "Kutokusema kwa yeyote."

dhabihu kwa utakaso wako

Sheria inamtaka mtu kufanya dhabihu maalumu baada ya utakaso wao. Hii ilimruhusu mtu kuwa safi kitaratibu, na kuweza tena kushiriki katika desturi kidini.

kwa ushuhuda

"Hii inathibitisha uponyaji wako""

Kwao

Maana zinazowezekana 1) "kwa makuhani" 2) "kwa watu wote"

Luke 5:15

Taarifa kumhusu yeye

"habari kuhusu Yesu." Hii pengine ingemaanisha "taarifa kuhusu uponyaji mtu kwa Yesu" au "taarifa kuhusu Yesu kuponya watu."

taarifa kuhusu yeye zilisambaa zaidi na zaidi

"taarifa kuhusu yeye zilizagaa sana" au "watu waliendelea kuzisema habari kuhusu yeye katika maeneo mengine"

maeneo yaliyotengwa

"maeneo ya pekee" au "maeneo ambapo hapakuwa na watu wengine"

Luke 5:17

Kauli Unganishi:

Siku moja Yesu alipokuwa akifundisha katika jengo, baadhi ya watu walimleta mtu aliyepooza kwaajili Yesu kumponywa.

Ilitokea

Kauli hii inaonesha mwanzo wa sehemu mpya katika simulizi.

Luke 5:18

Sasa baadhi ya watu wakaja

Hawa ni watu wapya katika simulizi. Lugha yako inaweza kuwa na njia ya kuonesha kwamba hawa ni watu wapya. "kulikuwa na watu ambao walikuja."

godoro

"kitu cha kulalia" au "kitu cha kuunyosha mwili"

alikuwa amepooza

"hangeweza kuondoka mwenyewe"

Wasingeweza kupata njia ya kumleta ndani kwa sababu ya kusanyiko, hivyo

Katika baadhi ya lugha inaweza inaweza ikawa kiasili ukirekebishwa. "Lakini kwa sababu ya mkutano wa watu, wasingepata njia kumleta mtu ndani"

kwasababu ya mkutano

Ni wazi kwamba sababu iliyowafanya wasiweze kuingia ilikuwa hadhara kubwa sana pale hapakuwa na nafasi kwaajili yao.

walikwenda juu hadi juu kabisa ya nyumba

Nyumba zilikuwa na dari, na baadhi ya nyumba zilikuwa na ngazi au kipandio (daraja) cha kurahisisha kupanda kule juu.

mbele ya Yesu kabisa

"mbele ya Yesu moja kwa moja" au "kwa haraka mbele ya Yesu"

Luke 5:20

angalia imani yao, Yesu alisema

ilieleweka kwamba walimwamini Yesu anaponya mtu aliyepooza. NI: "Yesu alipotazama kwamba wanaamini kwamba anaweza kumponya mtu, alimwambia "

Mwanadamu

Hili ni neno lililotumika kwa ujumla ambalo watu walitumia walipokuwa wakizungumza mtu na ambaye jina lake hawakulijua. ilikuwa siadabu, lakini pia haikuonesha heshima maalumu. Baadhi ya lugha ziliweza kutumia neno kama "rafiki" au "mkuu."

dhambi zako zimesamehewa

"umesamehewa" au "nasamehe dhambi zako"

hoji hiki

"jadili hili" au "toa hoja kuhusiana na hili." NI: "pengine jadili hata siyo Yesu alikuwa na mamlaka ya kusamehe dhambi."

Nani huyu ambaye anasema kufuru?

Swali hili linaonesha jinsi walivyoshituka na kukasirika kwa kile ambacho Yesu alisema. "Mtu huyu anamkufuru Mungu" au "Yeye anamkufuru Mungu kwa kusema hivyo"

Nani anayeweza kusamehe dhambi, lakini Mungu pekee?

Inachodokeza taarifa ni kwamba kama mtu anadai kusamehe dhambi anasema ni Mungu. "Hakuna anayeweza kusamehe dhambi lakini Mungu pekee" au "ni Mungu pekee ambaye anaweza kusamehe dhambi."

Luke 5:22

kutambua walichokuwa wanafikiri

Kirai hiki kinaashiria kwamba walikuwa wanahojiana kimya kimya, hivyo kwamba Yesu alitambua zaidi na alisikia walichokuwa wanfikiri.

Kwa nini mnaulizana hili mioyoni mwenu

Msingepaswa kusema hivi mioyoni mwenu " au"Msingepaswa kutia shaka kwamba nina mamlaka ya kusamehe dhambi"

Mioyoni mwenu

Hii inarejea sehemu ya mtu ambayo hufikiri au huamini.

rahisi kusema

Kitu ambacho hakipo wazi ni kimoja. "Ni rahisi kusema, sababu hakuna mmoja atakayejua, lakini kitu kingine ni "kigtumu kusema sababu kila mmoja atajua". watu wasione kama mtu dhambi zako zimesamehewa, 'lakini Mungu pekee anaweza sababisha huyu mlemavu kusimama na kutembea."

mnaweza kujua

Yesu alikuwa akiongea kwa Waandishi na Mafarisayo. Neno "enyi" ni wingi.

Mwana wa Adam

Yesu alikuwa akirejea yeye peke yake

Nasema kwenu

Yesu alikuwa akisema haya kwa mtu aliyepooza .Neno "wewe" ni umoja

Luke 5:25

kwa haraka

"mara moja"njia sahihi"

akainuka

Inaweza kusaidia kusema kwa wazi kwamba aliponywa. NI: "mtu aliponywa! akainuka."

kujawa na hofu

"hofu sana"au" kujawa na utisho"

vitu vinavyozidi vya kawaida

"vitu vya kushangaza "au" vitu vigeni"

Luke 5:27

Sentensi Unganishi:

Yesu alipoondoka nyumbani, anamwita Lawi, Myahudi mtoza ushuru amfuate. Lawi anaandaa mlo kwaajili ya Yesu uliowakera mafarisayo na waandishi.

Baada ya mambo hayo kutokea

Kirai "vitu hivi" kinamaanisha kilichotokea kwenye mistari iliyopita. Ishara hii ni tukio jipya.

akamwona mtoza ushuru

"akamwangalia mtoza ushuru kwa umakini "au" alimwangalia mtoza ushuru kwa uangalifu"

Nifuate

Kufuata mtu ilikuwa ni kauli imaanishayo kuwa mwanafunzi. NI: "Kuwa mwanafunzi wangu "au" njoo, nifuate kama mwalimu wako"

Acha vyote nyuma

"akaacha kazi yake kama mtoza ushuru"

Luke 5:29

Sentensi Unganishi

Chakulani, Yesu anazungumza na Mafarisayo na waandishi.

Nyumbani mwake

"kwenye nyumba ya Lawi"

walioketi mezani

Aina ya Kigiriki ya kula kwenye karamu ilikuwa kuegemea kochi na kujihimili peke yako kwa mkono wa kushoto kwenye baadhi ya mito ." au " "kwenye meza"kukaa mezani"

kwa wanafunzi wake

"kwa wanafunzi wa Yesu"

Kwa nini unakula ... kwa mtu mwenye dhambi?

Mafarisayo na Waandishi waliuliza haya kudhihirisha kutoridhishwa kwao kwamba Yesu na wanafunzi wake walikuwa wanakula na wenye dhambi. NI: "Huwezi kula na wenye dhambi!"

mnakula na kunywa pamoja ... watu wenye dhambi

Mafarisayo na waandishi waliamini kwamba watu wa dini wanapaswa kujitenga na watu waliowaona kuwa ni wenye dhambi. Neno "wewe" ni wingi.

Watu ambao ni wazima ... wagonjwa

Yesu anadhihirisha hii kama mithali.

Tabibu

daktari atibuye " au" daktari"

ni ambao wanaumwa tu

Maneno "inahitaji" yanaeleweka kutoka kirai kilichotangulia. NI: "ni wale wagojwa tu wanamwitaji"

watu wenye haki

Baadhi ya watu walifikiri wanahaki. Yesu anarejea kwa hao kwa namna walivyofikiri kuhusu wao wenyewe ingawaje alijua kwamba hawakuwa wenye haki. NI: "watu wafikirio wanahaki"

Luke 5:33

Akawaambia

"Viongozi wa dini wakasema kwa Yesu"

inawezekana yeyote akafanya ... pamoja nao?

Yesu alitumia swali kusababisha watu kufikiri kuhusu hali ambayo tayari wanaijua."Hakuna mmoja wenu anawaambia waliohudhuria harusini kufunga wakati bado Bwana arusi yupo nao."

waliohudhuria harusini

"wageni" au "marafiki. "Hawa ni marafiki ambao husherehekea na mtu ambaye anafunga ndoa.

waalikwa wa bwana arusi wanafunga

kufunga ni ishara ya huzuni. Viongozi wa dini walielewa kwamba waalikwa arusini hawawezi kufunga wakati bwana arusi akiwa pamoja nao.

siku zitakuja

"upesi" au siku hizo" (UDB)

Bwana Arusi atakapoondolewa kwao.

Yesu anajifananisha yeye mwenyewe na bwana arusi, wanafunzi wake ni waalikwa arusini. Hakufafanua sitiari, hivyo tafsiri ieleze kama ni lazima tu.

Luke 5:36

Taarifa kwa ujumla

Yesu anasema habari kwa waandishi na mafarisayo waliokuwa nyumbani kwa Lawi.

Hakuna mtu huchana

"Hakuna mmoja hupasua " au" mtu hachani kamwe"

kama alifanya hivyo

Kauli hii tete inaelezea sababu kwa nini mtu hatarekebisha vazi kwa njia hiyo.

kurekebisha

"karabati"

kisingefaa

"kisingeweza kukubaliana " au" kisingekuwa sawa"

Luke 5:37

Hakuna mtu awekae

"Mtu hawezi kuweka "au" hakuna hata mmoja huweka"

Divai mpya

"juisi ya dhabibu."Hii inamaanisha divai ambayo bado hajachachishwa."

Kiriba

Hii ni mifuko iliyotengenezwa kwa ngozi ya mnyama. Ingeweza kuitwa mifuko ya divai "au "mifuko iliyotengenezwa kwa ngozi."

kiriba kipya kingepasua ngozi

Kipindi divai mpya inachana na kuvutika, inapasua ngozi ya zamani kwa sababu hata hivyo hunyooka. Wasikilizaji wa Yesu walielewa taarifa zihusuzo divai iliyochachishwa na kuvutika.

Divai ingevuja

"Divai ingevuja nje ya mifuko"

viriba vipya

"viriba vipya " au "mifuko mipya ya divai."Hii inamaanisha viriba vipya vya divai, visivyotumika.

kunywa divai ya zamani ... anataka mpya

Sitiari hii inakanusha mafundisho ya zamani ya viongozi wa dini ni kinyume na mafundisho mapya ya Yesu. Dokezo ni kwamba watu ambao walizoea mafundisho ya zamani hawako tayari kusikiliza vitu vipya ambavyo Yesu anafundisha.

Divai ya zamani

"divai ambayo imechachishwa"

Anasema cha zamani ni bora

Itasaidia kwa kuongeza: na "hata hivyo tayari kujaribu divai mpya.

Luke 6

Luka 06 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Luka 6:20-49 ina baraka na ole nyingi ambazo zinaonekana kuwa sawa na Mathayo 5-7. Sehemu hii ya Mathayo kwa kawaida inaitwa "Mahubiri ya Mlimani." Katika Luka, hayashikamani na mafundisho juu ya ufalme wa Mungu kama katika injili ya Mathayo. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#kingdomofgod)

Dhana maalum katika sura hii

"Kula nafaka"

Ilikuwa nazoezi yaliokubaliwa kwa wasafiri kuchuma na kula kiasi kidogo cha nafaka kutoka kwa mimea katika mashamba waliyoyapitia. Sheria ya Musa ililazimisha walimaji waruhusu wasafiri hivyoo. Wafarisay waliwaza kama kuchuma nafaka ni kazi ya "kukusanya masuke yaiyobaki" na sheria ya Musa inazuia kufanya kazi kwa siku ya Sabato. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lawofmoses, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#works and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sabbath)

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Maneno yanayoonyesha mfano

Ilikuwa kawaida kwa Yesu kutumia maneno ya mifano kwa kufundisha watu ukweli usiyo rahisi wa kiroho. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

Maswali ya uhuishaji

Yesu alitumia maswali ya uhuishaji ili kuwafundisha watu na kuwahukumu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-rquestion)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Maelezo yaliyodokezwa

Mara nyingi Luka anaandika habari yaliyoelewa kabisa na watu wa kale wa inchi za Mashariki ya Karibu lakini labda watu wa leo wa mazoezi tofauti hawaelewi. kwa mfano watu wanatarajia siku ya hukumu ya mwisho au labda hukumu kwa siku ya mwisho ya maisha yao (Luka 6:37). (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

Wanafunzi kumi na wawili

Yafuatayo ni orodha ya wanafunzi kumi na wawili: Katika Mathayo: Simoni (Petro), Andrea, Yakobo mwana wa Zebedayo, Yohana mwana wa Zebedayo, Filipo, Bartholomayo, Tomasi, Mathayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni mzeloti na Yuda Iskarioti.

Katika Marko: Simoni (Petro), Andrea, Yakobo mwana wa Zebedayo na Yohana mwana wa Zebedayo (ambaye aliwaita Boanerge, yaani, wana wangurumo), Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomasi, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni mzeloti, na Yuda Isikarioti.

Katika Luka: Simoni (Petro), Andrea, Yakobo, Yohana, Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomasi, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni (aitwaye mzeloti, Yuda mwana wa Yakobo, na Yuda Isikarioti.

Inawezekana kuwa Thadayo na Yuda, mwana wa Yakobo, ni majina mawili ya mtu mmoja.

<< | >>

Luke 6:1

Sentensi Unganishi:

Sasa Yesu na wanafunzi wake wanatembea kupitia kwenye shamba la ngano wakati baadhi ya mafarisayo wanaanza kuwauliza wanafunzi kuhusu walichokuwa wanafanya siku ya sabato ambayo katika sheria ya Mungu imetengwa kwaajili ya Mungu.

Taarifa kwa Ujumla

Neno "wewe" hapa ni wingi, na linarejea kwa wanafunzi.

sasa ikatokea

Kirai hiki kilitumika hapakuzingatia mwanzo wa sehemu mpya ya masimulizi. Ikiwa lugha yako ni njia ya kufanya hivi, ingeweza kutumika hapa.

masuke

Kwa suala hili, hizi ni sehemu kubwa za nchi ambapo watu walikuwa wametawanya mbegu pawe na ngano nyingi.

juu ya ngano

Hii ni sehemu ya juu ya mmea wa ngano, ambao ni aina jani kubwa. inashikilia mbegu inayoota ya mmea.

kufikicha katikati ya mikono yao

Walifanya hivi kutenganisha ngano. NI: "Walifikicha ngano katika mikono yao kutenganisha ngano na ganda" (UDB)

Kwa nini mnafanya vitu ambavyo ni kinyume kufanya siku ya sabato?

Hili ni swali linalowatuhumu wanafunzi kwa kuvunja sheria. NI: "Kuchuma nafaka siku ya sabato ni kinyume na sheria ya Mungu!"

kufanya kitu fulani

Mafarisayo waliona hata kitendo kidogo cha kufikicha ngano kuwa ni kazi ivunjayo sheria. NI: "kufanya kazi"

Luke 6:3

Hamkuwahi hata kusoma ... yeye?

Yesu anawakemea mafarisayo kwaajili ya kutojifunza maandiko. Hii inaweza kuandikwa kama sentensi NI: "Mtajifunze kutokana na yale mliyo soma .... yeye"

Mkate wa wonyesho

"Mkate mtakatifu " au "mkate ambao uliokuwa ukitolewa sadaka kwa Mungu"

Mwana wa Adam

Yesu alikuwa anarejea yeye peke yake. 'Mimi' Mwana wa Adam. NI: "Mimi, Mwana wa Adamu"

ni Bwana wa Sabato

Cheo "Bwana" hapa inasisitiza mamlaka juu ya Sabato. NI: "ana mamlaka kutambua kipi ni sahihi kwa mtu kufanya siku ya sabato!"

Luke 6:6

Sentensi Unganishi:

Waandishi na Mafarisayo wanatazama Yesu anaponya mtu siku ya Sabato

Taarifa kwa Ujumla

Hapa sasa ni siku ya Sabato nyingine na Yesu yuko kwenye Sinagogi.

Ilitokea

Kirai hiki kimetumika hapa kuzibgatia mwanzo wa tukio jipya katika masimulizi.

Mtu alikuwa pale

Hii inatambulisha mhusika mpya kwenye simulizi.

mkono wake umepooza

mkono wa mtu ambaye umepata umeadhirika kiasi ambachomhawezi kuunyoosha. Ulikuwa umejikunja kwenye eneo la ngumi, ikaufanya uonekane mdogo na wenye kupinda.

walikuwa wanamuangalia kwa karibu

"walikuwa wanamuangalia Yesu kwa makini"

ili waweze kupata

"kwa sababu walitaka kutafuta"

katikati ya kila mmoja

"mbele ya kila mtu" (UDB). Yesu alimtaka yule mtu kusimama ambapo kila mmoja angemuona.

Luke 6:9

Kwao

"kwa Mafarisayo"

ni halali ... okoa maisha ... iharibu?

Yesu alitaka kuwasahihisha Mafarisayo wajuao kwamba ni kosa kuponya siku ya Sabato. Aliuliza swali kama kupinga kati ya kufanya wema au uovu ili kwamba iwe wazi kipi ni sahihi na kipi ni kibaya. NI: "tendo lipi ambalo sheria inaruhusu - kufanya wema na kuponya, au kuumiza na kuharibu maisha?"

kufanya mema au kufanya madhara

"kusaidia mtu au kumdhuru mtu"

Nyoosha mkono wako

"Shikilia mkono wako" au" panua mkono wako"

alirejeshwa

"aliponywa"

Luke 6:12

taarifa kwa Ujumla

Yesu anachagua mitume kumi na wawili baada ya kuomba usiku mzima.

Ikatokea katika siku hizo

kirai hiki kimetumika hapa kuashiria mwanzo wa kipande kipya cha masimulizi.

katika siku hizo

"katika wakati huo" au"sio mbali baada ya hapo " au" siku moja katikati ya hapo"

alikwenda nje

"Yesu alikwenda nje"

ilipokuwa siku

"ilipokuwa asubuhi" au "siku iliyofuata"

Aliwachagua kumi na wawili miongoni mwao

"aliwachagua kumi na wawili kati ya wanafunzi"

"ambao pia aliwaita mitume"

"ambao aliwafanya mitume" au "na alipowateua wao kuwa mitume."

Luke 6:14

majina ya mitume yalikuwa

Hizi ni taarifa zimeongezwa kwenye mstari wa ULB

ndugu yake Andrea

"kaka yake Simoni, Andrea"

Zelote

inawezekana maana 1) "Zelote" ni cheo kinacho onesha alikuwa sehemu ya kundi la watu waliotaka kuwaacha huru Wayahudi kutoka utawala wa Rumi NI: "mzalendo" au "mtaifa" au 2) "mwenye bidii" ni maelezo yanayoashiria alikuwa na bidii kwaajili ya Mungu kuheshimiwa. NI: "shauku"

kuwa msaliti

Inaweza kuwa lazima kueleza nini maana ya "msaliti" katika mkutadha huu. NI: "aliwasaliti rafiki zake" au "aliwageuka rafiki zake mbele ya maadui" (kawaida kwa kurudisha fedha alizolipwa" au "kumweka rafiki katika hatari kwa kuwaambia maadui kuhusu yeye"

Luke 6:17

Sentensi Unganishi:

Ingawa Yesu akiwaelekea hasa wanafunzi wake, walikuwapo watu wengi karibu ambao wanasikiliza.

pamoja nao

"pamoja na kumi na wawili aliowachagua" au "pamoja na mitume wake kumi na wawili"

waliponywa

Hii inaweza kusema katika kauli tendaji "kwa Yesu kuwaponya wao"

waliokuwa wakisumbuliwa na roho wachafu pia walipona

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. NI: "Yesu pia aliwaponya watu walisumbuliwa na roho wachafu."

waliosumbuliwa na roho wachafu

"sumbuliwa na roho chafu" au waliotawaliwa na roho chafu"

nguvu za kuponya zilikuwa zikimtoka

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji NI: "alikuwa na nguvu kuponya watu" au "alitumia nguvu zake kuponya watu"

Luke 6:20

Ninyi mmebarikiwa

Kirai hiki kimerudia mara tatu. Kila mara ,kinaashiria kwamba Mungu huwapa neema watu fulani au kwamba hali zao ni chanya au nzuri.

Mmebarikiwa ninyi mlio maskini

"Wale ambao ni maskini hupokea neema ya Mungu" au " ambao ni maskini hunufaika"

Kwa maana ufalme wa Mungu ni wenu

Lugha ambazo hazina neno ufalme laweza sema, "Mungu ni mfalme wako" au "kwa sababu Mungu ni mtwala wako."

Ufalme wako ni wa Mungu

"ufalme wa Mungu ni wako." Hii ingeweza kumaanisha 1) "umetokana na ufalme wa Mungu" au 2) Utakuwa na mamlaka katika ufalme wa Mungu."

Mtacheka

"Mtacheka na kufurahia" au "Mtakuwa na furaha"

Luke 6:22

Mmebarikiwa ninyi

"Mmepokea neema ya Mungu" au "Mnanufaika" au "Ni kwa namna gani ni nzuri kwenu"

Kuwatenga ninyi

"kuwakataa ninyi"

Kwa ajili wa Mwana wa Adam

"kwa sababu mnajumuika na Mwana wa Adam" au" kwa sababu walimkataa Mwana wa Adam "

Siku hiyo

"Kipindi wanafanya mambo hayo" au "kipindi yanatokea"

vuna kwa furaha

Nahau hii inamaanisha "kuwa na furaha zaidi"

dhawabu kubwa

"malipo makubwa" au "zawadi nzuri"

Luke 6:24

Ole wenu

"jinsi gani kwenu ni hatari." Kirai hiki kimerudia mara tatu. Ni kinyume cha "mmebarikiwa ninyi" Kila mara, kinaashiria kwamba hasira ya Mungu ni moja kwa moja kwa watu, au kwamba kitu hasi au kibaya kinawasubiri.

ole wenu ninyi mlio matajiri

namna gani balaa ni wale ambao ni matajiri" au "shida zitakuja kwa wale ambao ni matajiri"

Mfariji wenu

"mfariji wenu" au "kinacho waridhisha ninyi" au "kinacho wafanya mwe na furaha"

Mlio shiba sasa

"ambao matumbo yao yameshiba sasa" au "ambaye hula kingi sasa"

wanao cheka sasa

"ambaoana furaha sasa."

Luke 6:26

Ole wenu

"ni gani balaa gani litakuwa kwenu" au "jinsi mtakavyo kuwa na huzuni"

Kipindi wanadamu wote

kipindi watu wote" au "kipindi kila mmoja"

hivyo ndivyo wahenga waliwafanya manabii wa uongo

"walinena vizuri juu ya manabii wa uongo"

Luke 6:27

Sentensi Unganishi:

Yesu anaendelea kuzungumza kwa wanafunzi wake na vile vile na mkutano wanao msikiliza yeye.

kwenu mnaosikiliza

Yesu sasa anaaza kuzungumza kwa hadhara yote, zaidi kuliko kwa wanafunzi wake tu.

penda ... fanya mema ... Bariki ... omba

Katika kila amri hizi hufanyika kwa mwendelezo, siyo tu kwa mara moja.

penda adui zako

Hii hainamaana unawapenda tu adui na siyo marafiki. Hii inaweza kusemwa. NI: "Wapende adui, siyo tu rafiki!" (UDB)

penda ... fanya mema kwa

Virai viwili hivi vinamaana sawa, na kwa pamoja vinasisitiza hoja.

Bariki ambao

Mungu ndiye abarikie. Hii inaweza ikadhihirisha. NI: "Omba Mungu kubariki hao" (UDB)

ambao wanakulaani

"ambao wanatabia ya kukulaani"

wale ambao wanakutendea mabaya

"wale ambao wanatabia ya kukutenda mabaya"

Luke 6:29

Kwa yeye akupigaye

"kama yeyote akupigaye"

katika shavu moja

"kwenye upande mmoja wa uso"

Mpe pia upande mwingine

Inasaidia kusema ambacho mshambuliaji atafanya kwa mtu. NI: "geuza uso wako kwamba aweza kupiga na shavu jingine pia"

Usizuie

"hapana kumzuia kuchukua"

Mpe kila mmoja akuombaye

"Ikiwa yeyote anakuomba kitu, mptie"

usimuulize

"usimwombe" au "usihitaji"

Luke 6:31

Kama unavyotaka watu wakufanyie, ufanye hivyo kwao

Kwa baadhi ya lugha zingine inaweza kuwa uasilia zaidi kubadili amri: NI: "Uwafanyie watu sawasawa na unavyotaka watu wakufanyie."

Ni ujira gani kwenu?

"Ni dhawabu gani mtapokea?" au "Mtapokea sifa gani kwa kufanya hivyo?" Hii inaweza kuandikwa kama sentensi. NI: "Hamtapokea thawabu yeyote kwa hilo" au "Mungu hatawazawadia kwa hilo"

kurudisha kiasi kile kile

Sheria ya Musa iliamuru Wayahudi wasipokee riba kwa pesa waliyokopeshana.

Luke 6:35

Dhawabu yenu itakuwa kubwa

"mtapokea dhawabu kubwa" au "mtapokea malipo mazuri" au "mtapata zawadi nzuri kwa sababu ya hilo"

Mtakuwa wana wa aliye juu

Ni vizuri sana kutafsiri "wana" kwa maneno ambayo lugha yako itayatumia kwa asili kurejea kwa mwana wa kibinadamu.

wana wa aliye juu

Hakikisha kwamba neno "wana" ni wingi lisichanganywe na cheo cha Yesu "Mwana wa aliye Juu Sana"

Wasio na shukrani na ni watu waovu

"Watu ambao hawamshukuru yeye na ambao ni waovu"

Baba yako

Hii inamrejea Mungu. Ni bora kutafsiri "Baba" kwa neno ambalo lugha ambayo kwa asili hutumika kurejea kwa baba binadamu.

Luke 6:37

Msihukumu

"Msihukumu watu" au "usimkosoe mtu"

na wewe

"na kama matokeo yako"

hamtahukumiwa

Yesu hakusema ambao wasingehukumu. Inawezekana maana ni 1) "Mungu hatakuhukumu wewe" au 2) "hakuna wa kukuhukumu wewe."

Msishutumu

"Msishutumu watu"

Hamtashutumiwa

Yesu hakusema ambaye angehukumu. inawezekana inamaanisha 1) "Mungu hatakushutumu wewe" au 2) "hakuna hata mmoja atakaye washutumu."

Nanyi mtasamehewa

Yesu hakusema ambaye angesamehe. Inawezekana inamaanisha 1) "Mungu atakusamehe" au 2 ) "watu watakusamehe."

Luke 6:38

Nanyi mtapewa

Yesu hakusema kwa hakika ambaye angetoa. Inawezekana inaanisha 1) "yeyote atakupa wewe 2) "Mungu atakupa wewe?

kiasi cha ukarimu ....magotini penu

Amri ya sentensi hii inaweza kurudiwa. NI: "kitamwagwa magotini penu kiasi cha ukarimu kilichosindiliwa na kumwagika. "Yesu alitumia mfano wa mfanya biashara wa nafaka kupata kiasi cha ukarimu. NI: "Ni kama mfayabiashara wa nafaka ambaye hushindilia nafaka na kuzitikisa pamoja na hutoka nafaka nyingi ambazo humwagika, watakupatia wewe kwa ukarimu.

Kiasi cha ukarimu

"kiasi kingi"

Itapimwa hivyo hivyo kwako

Yesu hakusema kwa hakika nani atapima. Maana zinazowezekana 1)"watatumia kipimo hicho hicho kupima vitu vyako" au 2) Mungu atakupimia pia vitu wewe

Luke 6:39

Sentensi Unganishi

Yesu anahusisha baadhi ya mifano kujenga hoja yake.

mtu kipofu anaweza kumuongoza kipofu mwingine?

Yesu alitumia swali ili kupata watu wa kufikiri kitu ambacho tayari wanajua. Hii inaweza kuandikwa kama sentensi. NI: "Mtu kipofu hawezi kumuongoza mtu mwingine kipofu.

mtu kipofu

mtu ambaye ni "kipofu" ni sitiari kwa mtu ambaye hajafundishwa kama mwanafunzi.

Ikiwa alifanya

Baadhi ya lugha zinaweza kupendelea, "kama mmoja alifanya" Hii ni hali upuuzi kwamba haiwezi kabisa kutokea.

wote wataangukia shimoni, je hawawezi?

Hii inaweza kuandikwa kama sentensi. NI: wawili wote wataangukia shimoni"

Mwanafunzi siyo mkubwa kuliko mwalimu mwalimu wake

"Mwanafunzi hawezi kumzidi mwalimu wake." Maana zinazowezekana ni 1) "Mwanafunzi hana maarifa kuliko mwalimu wake" au 2) Mwanafunzi hana mamlaka kuliko mwalimu"

Mwanafunzi hawi mkubwa kuliko mwalimu wake

Hii inaweza kumaanisha kuwa 1)"mwanafunzi hawezi kuwa na ufahamu mkubwa kuliko mwalimu "au 2) " Mwanafunzi hana mamlaka zaidi ya mwalimu ."Mwanafunzi hawezi kumzidi mwalimu."

kila mmoja akishamaliza kufundishwa

"Kila mwanafunzi aliyefundishwa vizuri" au "kila mwanafunzi ambaye amejazwa mafundisho na mwalimu."

Luke 6:41

kwanini unaangalia ... lakini huzingatii kijiti ambacho kimo kwenye jicho lako?

Yesu anatumia swali hili kuwapa watu changamoto kuzingatia dhambi zao wenyewe kabla hawajafuatilia dhambi za watu wengine. NI: "usiangalie ... lakini puuza kitiji ambacho kimo kwenye jicho lako"

kibanzi kilichomo kwenye jicho la ndugu yako

Hii ni sitiari ambayo inarejea kwenye kosa dogo alilofanya muumini mwenzako.

kipande cha kijiti

"doa" (UDB) au "kibanzi." Tumia neno kwa kitu kidogo ambacho kwa kawaida kinaingia kwenye jicho la mtu.

ndugu

Hapa "ndugu" inanarejea kwa myahudi au muumini mfuasi wa Yesu.

kijiti ambacho kimo kwenye jicho lako

Hii ni sitiari kwa kosa la mtu maarufu. kijiti hakiwezi kuingia kwenye kwenye jicho la mtu kilivyo. Yesu anasisitiza kwamba mtu awe makini kwa makosa yake mwenyewe kabla hajashughulikia makosa madogo ya mwingine.

kijiti

"boriti " au "kigogo"

Unawezaje kusema ... jicho?

Yesu anauliza swali hili kukosoa watu wazingatie dhambi zao kabla ya kufuatilia dhambi za wengine. NI: "Usiseme ... jicho"

Luke 6:43

Taarifa kwa Ujumla:

watu wanaweza wakasema kama mti ni mzuri au mbaya, na ni aina gani ya mti, kwa matunda yake unayozaa. Yesu anatumia hii kama sitiari isiyo elezewa - tunajua mtu wa aina gani kwa ya kuona mtendo yao.

kwa kuwa ipo

"sababu ipo" Hii inaashiria kwamba kinachofuata ni sababu ni sababu ya kwanini hatupaswi kuwahukumu ndugu zetu

mti mzuri

mti wenye afya

haribika

"liooza" au "baya" au "siofaa"

Kila mti hujulikana

watu hutambua aina ya mti kwa matunda yake unayozaa. Hii inaweza kusemwa kwa kauli tendaji. NI: "watu wanajua aina ya mti" au "watu wanatambua mti"

Mchongoma

Mmea au kichaka chenye miiba

waridi mwitu

mzabibu au kichaka kilicho na miiba

Luke 6:45

Taarifa kwa Ujumla:

Yesu analinganisha mawazo ya mtu kwa hazina nzura au mbaya. Mawazo mazuri ya mtu mzuri yanasababisha matendo mazuri. Mawazo maovu ya mtu mwovu husababisha matendo mabaya.

Mtu mwema

Neno "mwema" hapa linahusu mwenye haki au maadili mema.

mtu mwema

Neno "mtu" linarejea kwa mtu, mwanaume au mwanamke. NI: "mtu mwema"

Hazina njema ya moyo wake

"vitu vizuri hutunza moyoni mwake" au "vitu vizuri huvithamini"

huzaa kilicho kizuri

Kutoa kilicho kizuri ni sitiari kwa kufanya mema. NI: "kufanya kilicho kizuri"

hazina mbaya ya moyo wake

"mambo mabaya anayotunza moyoni mwake" au "mambo mabaya anayothamini"

katika utajiri wa moyo wake mdomo huzungumza

Kirai "kinywa chake" kinawakilisha yeye kutumian mkinywa chake. NI: "anachofikiri moyoni mwake kinaathiri anachosema kwa mdomo wake" au anachokithamini moyoni mwake huamua kinachosemwa na kinywa.

Luke 6:46

Taarifa kwa Ujumla:

Yesu anamlinganisha mtu ambaye anatii na mtu anayejenga nyumba juu ya mwamba ambapo itakuwa na uimara na gharika.

Bwana, Bwana

Urudiaji wa maneno haya huashiria kwamba walimwita Yesu kwa kawaida "Bwana."

Kila mtu ajaye kwangu ... nitakwambia anacho kifanana

Itakuwa wazi zaidi kubadili mfumo wa sentensi hii. NI: "Nitakuambia jinsi kila mtu anayekuja kwangu akasikia na kuyatii maneno yangu anavyofanana "

jenga msingi wa nyumba kwenye mwamba imara

"Kuchimba msingi wa nyumba kwa kina kufikia mwamba imara" Baadhi ya tamaduni hawajengi juu ya mwamba, wanaweza kuhitaji kutumia kitu kingine kwa msingi imara.

Msingi

"msingi" au "saidia"

mwamba imara

Huu ni mwamba mgumu ambao upo chini ya udongo.

Maporomoko ya maji

"maji yaendayo kasi" au "mto "

Yakatokea dhidi

"Yakagonga dhidi yake"

tikisa

Maana zinazowezekana ni 1) "sababisha kutikisika" au 2) "iharibu."

Kwa sababu ilikuwa imejengwa vizuri

"kwa sababu mtu alikuwa ameijenga vizuri"

Luke 6:49

Taarifa kwa Ujumla:

Yesu anamlinganisha mtu asikiaye hatii mafundisho na mtu ambaye kajenga nyumba bila msingi hivyo itaanguka wakati wa mafuriko.

lakini mtu

"Lakini" inaonesha utofauti mkubwa kwa mtu aliyetangulia ambaye alijenga kwenye msingi.

juu ya ardhi pasipo msingi

Baadhi ya tamaduni nymba yenye msingi ni imara. Taarifa za kuongeza zinaweza zikawa msaada NI: "lakini hakuchimba chini na kujenga kwanza msingi"

Msingi

"msingi" au "msaada imara"

mafuriko ya maji

"maji -yanayotembea kwa kasi"

Maporomoka

"maji yanakwenda kwa kasi" au "mto"

tiririka kinyume

"iliyogonga"

poromoka

"anguka chini" au "ikagawanyika"

kifusi cha nyumba hiyo kilikuwa kamili

"nyumba hiyo ilikuwa imeharibika kabisa"

Luke 7

Luka 07 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri hupendelea kuweka mbele kidogo nukuu za Agano la Kale. ULB na tafsiri nyingine nyingi za Kiingereza huingiza mistari yote ya 7:27, ambayo ni nukuu kutoka Agano la Kale.

Kuna nyakati katika maelezo ya sura hii ambapo kuna mabadiliko ya ghafla katika mada. Mtafsiri hapaswi kulainisha mabadiliko haya.

Dhana maalum katika sura hii

Jemadari

Hali hii haikuwa jambo la kawaida sana katika Israeli ya kale. Haikuwa kawaida kwa askari wa Kirumi kuhitaji chochote kwa Waisraeli kwani hawakuwa wa maana kwa Warumi na hawangehitaji uponyaji kutoka kwa Myahudi. Haikuwa pia kawaida kwa tajiri kujali maslahi ya mtumwa wake. Hii inaonyesha imani kuu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith)

Ubatizo wa Yohana

Ubatizo ambao Yohana alifanya ulikuwa tofauti na ubatizo ambao kanisa linafanya. Ubatizo wa Yohana ulikuwa unaashiria kuwa wale waliopokea walikuwa wametubu dhambi zao. Ndio maana Mafarisayo hawakuhusika katika ubatizo wa Yohana. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#repent and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin).

"Wenye dhambi"

Luka anaashiria kundi la watu kuwa "wenye dhambi." Viongozi wa Kiyahudi waliona watu hawa kuwa hawaelewi Sheria ya Musa, na hivyo wakawaita "wenye dhambi." Kwa kweli, viongozi wenyewe ndio walikuwa wenye dhambi. Hali hii inaweza kuchukuliwa kama kinaya. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-irony)

"Miguu"

Miguu ilionekana kuwa ni chafu sana katika inchi za Mashariki ya Karibu ya Kale. Ingekuwa tendo la unyenyekevu sana kwa mwanamke huyu kuosha miguu ya Yesu na ilikuwa njia ya kumheshimu Yesu.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Mwana wa Binadamu"

Yesu anajiita mwenyewe kama "Mwana wa Binadamu." Lugha zingine haziwezi kuruhusu mtu kujitaja mwenyewe kama 'mtu wa tatu.' (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sonofman)

<< | >>

Luke 7:1

Taarifa kwa ujumla

Yesu anaingia Kapernaumu pale alipomponya mtumishi wa akida.

watu wakiwa wanasikiliza

Nahau "wakati watu wanasikiliza" anasisitiza anataka watu wasikie anchosema. NI: "ni kwa watu ambao walikuwa wanamsikiliza" au "kwa watu waliohudhuria" au "kwaajili ya watu kusikia"

Aliingia Kapernaumu

Hii inaanzisha tukio jipya katika simulizi

Luke 7:2

Nani alikuwa wa thamani kwake

"ambaye akida alimthamini" au "ambaye alimweshimu"

alimuuliza kwa uaminifu

"sihi pamoja" au "alimwomba"

anayestahili

"akida anastahili"

Taifa letu

"Watu wetu" hii inarejea kwa wayahudi.

Luke 7:6

aliendelea kwenye njia yake

"alienda"

siyo mbali kutoka kwenye nyumba

kauli hasi hizi zinaweza kubadilishwa. NI: "karibu na nyumba"

Usijisumbue mwenyewe

Akida alikuwa anaongea kwa upole kwa Yesu. NI: "Usijisumbue mwenyewe kwa kuja nyumbani kwangu" au "Sitaki kukuudhi"

Ingia chini ya dari yangu

Kirai hiki ni nahau inayo maanisha "Njoo ndani ya nyumba yangu." Kama lugha yako ina nahau inayomaanisha "Njoo kwenye nyumba yangu" fikiri kama ina weza kuwa nzuri kuweka hapa."

sema neno tu

Mtumishi alijua kuwa Yesu atamponya yule mtumishi kwa kusema tu. Hapa "neno" linarejea kuamuru. NI: "toa tu agizo"

Mtumishi wangu atapona

Neno lililotumiwa kutafsiri hapa kama "Mtumishi" mara nyingi limetafsiriwa kama "Mvulana" inaweza kuonyesha ishara kuwa mtumishi alikuwa kijana mdogo au inaonyesha ufanisi wa akida kwake.

kwa mtumishi wangu

Neno lililotafsiriwa hapa kama "mtumishi" ni neno la kawaida kwa mtumishi.

Luke 7:9

Alimshangaa

"alimshanga akida"

nawaambia

Yesu alisema haya kusisitiza maajabu ambayo anataka kuwaambia.

hata katika Israel sijawahi kuona imani kubwa hivi

maana yake ni kuwa Yesu alitarajia wayahudi kuwa na imani kama hii, lakini hawakuwa hivyo. Hakuwatajia wamataifa kuwa na imani ya namna hii, lakini huyu mtu amekuwa na imani hiyo. Unaweza kuongeza taarifa iliyofichika. NI: "sijaona mwisraeli yeyote anaye niamini kwa kiasi kama mmataifa huyu!" (UDB)

wale waliokuwa wametumwa

Ilifahamika kwamba hawa walikuwa watu waliotumwa na akida. Hii inaweza kusemwa NI: "watu ambao watawala wa Rumi waliowatuma kwa Yesu"

Luke 7:11

Sentensi Unganishi

Yesu anaenda katika mji wa Naini, pale alipomponya mtu aliyekuwa amekufa.

Naini

ni jina la Mji

tazama, mtu aliyekufa alikuwa kafa

Neno "Tazama" linatuashiria utangulizi wa simulizi ya mtu aliyekufa kwenye habari. Lugha yako inaweza kuwa na njia ya kufanya hivi. NI: "Kulikuwa na mtu aliyekufa"

mtu ambaye alikuwa amekufa alikuwa kabebwa

Hii inaweza ikasemwa katika kauli tendaji. NI: watu walikuwa wanapeleka nje ya mji mtu aliyekufa"

mwana pekee wa mama yake (ambaye alikuwa mjane)

"alikuwa mwana pekee wa mamaye, na alikuwa mjane" Hii ni taarifa iliyotangulia kuhusu aliyekufa na mama yake.

ilitokea kuwa

hii sentensi inatumika hapa kuonyesha mwanzo wa habari mpya. kama Lugha yako ina njia nyingine ya kufanya hivi unaweza kutumia hapa.

mjane

mwanamke ambaye mumewe amesha kufa

alisukumwa na huruma kwa ajili yake

"aliona huruma kwa ajili yake"

akaja mbele

"akaenda mbele" au "akamsogelea aliyekufa"

jeneza lililokuwa limebeba mwili

Hiyo ilikuwa ni machela au kitanda kilitumika kubeba mwili kwenda maeneo ya kuzika. kisingeweza kuwa kitu cha kuzikia. Tafsiri nyingine inapunguza uthamani "Jeneza" au "Kiti cha msiba"

nasema kwako

Yesu alisema hili kuonyesha mamlaka yake "Nisikilize!"

maiti

mtu alikuwa bado amekufa; sasa alikuwa hai. Itakuwa lazima kusema hili wazi. NI: "ni mtu aliyekuwa amekufa."

Luke 7:16

Sentensi Unganishi

Hii inatumabia jinsi ilivyotokea kama matokeo ya uponyaji wa Yesu kwa mtu aliyekuwa amekufa.

hofu ikawajaa wote

"Hofu huwajaa wote." Hii inaweza katika kauli tendaji. NI: "wate wakawa na hofu sana."

Nabii mkuu

Walikuwa wanarejea kwa Yesu, siyo kwa yule nabii asiyejulikana.

Ameinuliwa kati yetu

"Amekuja kuwa nasi" au "Ameonekana kwetu." Mungu ameinua nabii mkuu katikati yetu." Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. NI: "Mungu ameinua nabii mkuu kati yetu"

amengalia juu ya

Nahau hii inamaana "ajali"

Habari hizi njema kuhusu Yesu zikaenea

"Habari hizi njema" inarejea kwa vitu ambavyo watu walikuwa wanasema katika mstari wa 16. Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji "Watu wakaeneza hizi taarifa kuhusu Yesu" au "Watu waliwaambia wengine hii taarifa ya kuhusu Yesu."

Habari hizi

"Hili neno" au "Huu ujumbe"

Luke 7:18

Taarifa Unganishi :

Yohana anatuma wawili wa wanafunzi wake kumuuliza Yesu.

Wanafunzi wa Yohana walimwambia kuhusu mambo yote

Hii inatambulisha tukio jingine kwenye habari

akamwambia

"akamwambia Yohana"

mambo yote haya

"mambo yote alikuwa anafanya"

watu walisema, "Yohana mbatizaji ametutuma kwako kusema 'ni wewe ... au tumtazamie mwingine?"

Sentensi hii inaweza kuandikwa hivyo kwamba ikawa na nukuu ya moja kwa moja tu. NI: "watu walisema kwamba Yohana mbatizaji aliwatuma wao kwake kuuliza 'wewe ni yule ajaye, au tumtazamie mwingine?" au "watu walisema, '"Yohana katutuma sisi kwako kuuliza kama ni yule ambaye anakuja, au kama tutazamie mwingine."

tumtazamie mwingine

"tusubiri mwingine" au "tumtazamie mtu fulani"

Luke 7:21

Kwa saa hiyo

"kwa wakati huo"

kutoka kwa roho wachafu

Itakuwa msaada kusema tena uponyaji. NI: "aliwaponya na roho chafu"au "na aliwaweka huru watu kutoka katika roho chafu"

aliwaambia

"aliwaambia wajumbe wa Yohana" au "alisema kwa wajumbe aliowatuma Yohana"

Toa taarifa kwa Yohana

"Mwambie Yohana"

watu wahitaji

"watu masikini"

Mtu asiyeacha kuniamini kwa sababu ya matendo yangu amebarikiwa

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. NI: "Mungu atambariki mtu ambaye haachi kuamini kwake sababu ya matendo yake"

Mtu

"Watu" au "yeyote" Huyu si mtu maalumu.

usisitishe

maana mbili hasi "Hendelea"

Luke 7:24

Sentensi Unganishi

Yesu anaanza kuzungumza katika makutano kuhusu Yohana mbatizaji. anauliza maswli balagha kuwasaidia kufikiri kuhusu ambacho Yohana mbatizaji hasa anavyofanana.

Nini ... mwanzi ukutikiswa na upepo?

Hii inategemea jibu hasi. "milikwenda nje kuona mwanzi ukitikiswa na upepo? siyo hivyo" Inaweza pia ikaandikwa kama sentensi. NI: "Kwa hakika hamkwenda kuona mwanzi ukitikiswa na upepo!"

Mwanzi umetikiswa na upepo

Maana zinazowekeana kwa sitiari hii ni (1) mtu anaye badili mawazo yake, kama mwanzi ni rahisi kugeuzwa na upepo, au 2) mtu anayeongea sana lakini hasemi chochote cha mhimu, kama mwanzi ugeuzwavyo wakati upepo unapovuma.

Lakini nini ... mtu aliyevaa mavazi laini?

Hii pia inatazamia jibu hasi, sababu Yohana alivaa vazi gumu. "mlikenda huangalia mtu amevaa nguo laini? siyo hivy!" Hii pia inaweza kuandikwa kama sentensi. NI: Hakika hamkwenda kuona mtu amevaa nguo laini!"

liyevaa nguo laini

Hii inarejea nguo za gharama. Nguo za kawaida zilikuwa chakavu. NI "vaa nguo za gharama"

Ikulu ya mfalme

Ikulu ni kubwa, nyumba ya gharama anayoishi mfale.

Lakini ... Nabii?

Hii inaelekea kwenye jibu chanya. "Mlikwenda nje kuona nabii?" Ndivyo mlivyofanya!" Hii pia inaweza ikaandikwa kama sentensi. NI: "Lakini mlienda kweli kuona nabii!"

Ndiyo, asema kwenu

Yesu alisema kusisitiza umhimu wa vile ambavyo angesema badaye

zaidi ya nabii

Kirai hiki kinamaanisha kwamba Yohana alikuwa kabisa nabii, lakini kwamba alikuwa hata zaidi ya nabii halisi. NI: ""siyo nabii wa kawaida" au "ni muhimu zaidi ya nabii wa kawida"

Luke 7:27

Huyu ndiye aliyeandikiwa

"Nabii huyo ni yule manabii waliyeandika kumhusu" au "Yohana ni yule manabii walimwandika wakati mrefu uliopita"

Tazama, mimi namtuma

katika mstari huu, Yesu anamnukuu nabii Malaki na kusema kuwa Yohana ni mjumbe wa kile Malaki alisema.

Mbele ya uso wako

Nahau inamaana "Mbele yako" or "kwenda mbele yako"

yako

Neno "Yako" ni umoja kwa sababu Mungu aliongea kwa masihi katika nukuu.

Nasema kwako

Yesu alikuwa anaongea na makutano hivyo "Ninyi" ni wingi. Yesu alitumia kirai hiki kusisitiza ukweli wa vitu vya kushangaza aliokuwa anaenda kuusema.

kati ya waliozaliwa na mwanamke

"baadhi ya wale mwanamke amewazaa" hii ni sitiari lakini inalenga kwa watu wote. NI: "watu wote waliowahi kuishi."

Hakuna aliye mkuu kuliko John

"Yohana ni mkuu zaidi"

angalau mtu mhimu katika ufalme wa Mungu

Hii inahusiana na kila mtu ambaye ni sehemu ya ufalme ambao Mungu atauanzisha.

Ni mkuu kuliko alivyo

kiwango cha kiroho cha watu katika ufalme wa Mungu kitakuwa cha juu kuliko cha watu kabla ya ufalme uliokuwa umeanzishwa. NI: "kiwango cha kiroho cha juu kuliko Yohana"

Luke 7:29

Taarifa kwa Ujumla

Luka, mwandishi wa kitabu, alichangia juu ya mwitikio wa watu kwa Yohana na Yesu.

Wakati watu wote ... ubatizo wa Yohana

Mstari huu unaweza kurekebishwa wazi zaidi. NI: "wakati watu wote waliokuwa wamebatizwa na Yohana, wakiwemo watoza ushuru, walisikia hiki, wakatangaza kwamba Mungu ni mwenye haki.

walitangaza kuwa Mungu ni mwenye haki

"Walisema kwamba Mungu amejionyesha mwenyewe kuwa ni mwenye haki" au "walitangaza kuwa Mungu alitenda kwa haki

sababu walibatizwa na ubatizo wa Yohana

Hii inaweza ikasemwa katika kauli tendaji NI: "sababu walikubali Yohana awabatize" au "sababu Yohana aliwabatiza wao."

walikataa kusudi la Mungu kwa ajili yao wenyewe

"walikataa ambacho Mungu alitaka wao wafanye" au "chagua kutotii ambacho Mungu aliwaambia"

wao hawakubatizwa na Yohana

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji NI: "ambao Yohana hakuwabatiza" au "ambao walikataa kubatizwa na Yohana" au " wale waliokataa ubatizo wa Yohana."

Luke 7:31

Taarifa Unganishi:

Yesu aliendelea kusema kwa watu Kuhusu Yohana mbatizaji.

Tena, naweza kuwalinganisha na nini ... wanafanana?

Yesu alitumia maswali kutambulisha mlinganisho.Yawaeza kuandikwa kama sentensi. NI: "Hivi ndivyo nitawafananisha kizazi hiki., na ndivyo wanavyofanana.

Watu wa kizazi hiki

Watu wanalioishi wakati wa Yesu anasema

Wanafanana

Haya maneno ni mwanzo wa kulinganisha kwa Yesu. Yesu anasema kwamba watu wa kizazi hiki wanafanana na watoto ambao hawaridhiki na njia mbazo watoto wengine wanafanya

Eneo la soko

Kubwa, eneo la wazi ambapo watu huja kuuza bidhaa zao.

na hamkucheza

"Lakini hamkucheza kwenye mziki"

Na hamkuomboleza

"Lakini hamkuomboleza na sisi"

Luke 7:33

hakula mkate

Maana zinazowezekana ni 1) "Kufunga mfululizo" au 2) kutokula chakula cha kawaida

mnasema, 'Ana pepo'

Yesu alikuwa ananukuu kile watu walikuwa wanasema kuhusu Yohana. Hii inaweza ikasemwa bila nukuu ya moja kwa moja. NI: "Mlisema kuwa ana pepo" au "Mlimtuhumu kuwa ana Pepo"

Mwana wa Mtu

Yesu alitarajia watu pale kujua kuwa alikuwa anajisemea mwenyewe. NI: "Mimi" mwana wa mtu.

Mkasema, "Angali ... mdhambi"

Yesu alikuwa ananukuu kile watu walikuwa wanasema kuhusu mwana wa Mtu. Hii inaweza kusemwa moja kwa moja. NI: "mmesema kwamba mimi ni mtu Mlafi na mlevi, rafiki wa watoza ushuru na wenye dhambi"

Mtu mlafi

Ni yule kitabia ya hula chakula kingi zaidi ya uhitaji wake.

hekima imetambulika kuwa ina haki kwa watoto wake wote

Hii inaonekana kabisa kuwa ni mithali ambayo Yesu aliihusisha na hali hii. Hii huenda inamaana kwamba watu wenye hekima wangeelewa watu hawangemkataa Yesu na Yohana.

Luke 7:36

Sentensi Unganishi:

Mfarisayo alimwalika Yesu kula nyumbani kwake.

Taarifa kwa Ujumla

Ilikuwa ni desturi ya wakati huo mtazamaji kuhudhuria chakula cha jioni bila kula.

Sasa mmoja wa mafarisayo

Alama ya mwanzo mpya wa habari na inatambulisha mfarisayo kwenye habari.

aliegemea kwenye meza ili ale

"Alikaa kuzunguka kwenye meza kwa ajili ya chakula." Ilikuwa ni desturi kwa chakula cha starehe kama hiki chakula cha jioni kwa wanaume kula huku wakiwa wamejilaza kwa raha wakizunguka meza.

Tazama kulikuwa na mwanamke mmoja

Neno "Tazama" linatutazamisha sisi kwa mtu mwigine katika hadithi. Lugha yako inaweza ikawa na namna ya kufanya hivi.

aliyekuwa na dhambi

Yawezekana alikuwa kahaba. "Aliyeishi maisha ya dhambi" au "Ambaye alikuwa na sifa za kuishi maisha ya dhambi."

chupa ya manukato

"chupa hii ilitengenezwa kwa jiwe laini." Chupa ni laini, mwamba mweupe. watu walihifadhi vitu vya thamani katika hiyo chupa.

mafuta ya manukato

"na manukato ndani yake." manukato yalikuwa ni mafuta yaliyokuwa yanatoa harufu nzuri ndani yake. watu walijipaka wao wenyewe au kunyunyizia nguo zao ili wanukie vizuri.

kwa nywele za kichwa chake

"Kwa nywele zake"

kuwalowanisha kwa manukato

"mwaga manukato juu yao"

Luke 7:39

akawaza mwenyewe akisema

"alisema yeye mwenyewe"

Kama huyu mtu angekuwa nabii, angejua ... mdhambi

Farisayo aliwaza kuwa Yesu hakuwa nabii kwa sababu amemruhusu mwanamke mwenye dhambi kumgusa. NI: "Inaonekana Yesu siyo nabii, sababu nabii angejua kwamba mwanamke anayemgusa ni mwenye dhambi."

ni mdhambi

Simoni kimakosa alihisi kwamba nabii asingeruhusu kuguswa. Ukweli huu ungeongezwa. NI: "ni mdhambi na asingeruhusiwa kugusa"

Simoni

Hili lilikuwa ni jina la Farisayo aliyemwalika Yesu katika nyumba yake. Huyu hakuwa Simoni Petro.

Luke 7:41

Taarifa kwa Ujumla:

Kusisitiza nini anaenda kumwambia Simoni Farisayo, Yesu alimwambia hadithi.

Kulikuwa na wadaiwa wawili kwa mkopeshaji mmoja

"mkopeshaji fulani alikuwa na wadeni wawili"

dinari mia tano

"posho ya siku 500. " Dinari" ni wingi wa dinarius." Dinari ilikuwa ni sarafu ya fedha.

hamsini

"posho ya siku 50"

aliwasamehe wote

"aliwasamehe madeni yao" au "aliyafuta madeni yao"

Nadhani

Simoni alikuwa na tahadhari ya jibu hili. NI: "Huenda"

Umehukumu kwa usahihi

"Uko sahihi"

Luke 7:44

Yesu akamgeukia mwanamke

"Yesu akamwangalia mwanamke. "Yesu akaelekeza uamkini wa Simoni kwa mwanamke kwa kumgeukia"

hukunipa maji kwaajili ya miguu yangu

Huu ni wajibu wa msingi kwa mwenyeji kuleta maji na taulo kwaajili ya wageni kuoshwa na kukausha miguu yao baada ya kutembea kwenye njia ya vumbi.

wewe ... lakini yeye

Yesu mara mbili anatumia virai hivi kupinga upungufu wa heshima ya Simoni kwa kile kitendo cha ziada cha mwanamke.

kailowanisha miguu yangu kwa machozi yake

Mwanamke alitumia machozi yake kwa maji yaliyokosekana.

aliifuta kwa nywele zake

Mwanamke alitumia nywele zake badala ya taulo iliyokosekana.

hukunipa busu

"Mwenyeji mzuri kwenye huo utamaduni aliwasalimia wageni wake kwa busu kwenye shavu. Simono hakufanya."

hakuacha kunibusu miguu yangu

"ameendelea kunibusu miguu yangu"

Luke 7:46

Hukufanya ... lakini yeye

Yesu anaendelea kupinga wema hafifu wa Simoni na kitendo cha mwanamke

tia kichwani pangu mafuta

"paka kichwa changu kwa mafuta" Hii ilikuwa ni desturi ya kumkaribisha mgeni aliyeheshimika. NI: "nikaribisha kwa kunitia mafuta kichwani"

tia mafuta miguu yangu

Mwanamke alimweshimu sana Yesu kwa kufanya hivi. Alitoa kielelezo cha unyenyekevu kwa kutia mafuta miguuni badala ya kichwani.

Nawaambia

Hii inasisitiza umhimu wa sentensi inayofuata.

dhambi zake, ambazo zilizo nyingi, zimesamehewa

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. NI: "Mungu kasamehe dhambi zake nyingi"

yeye alipenda zaidi

upendo wake ulikuwa ulikuwa ushahidi kwamba dhambi zake zimesamehewa. Baadhi ya lugha zinahitaji kitu cha "Upendo" Kusema. "alipenda zaidi ambaye amemsamehe" au " alimpenda sana Mungu."

Lakini aliyesamehewa kidogo

"Mtu yeyote anasamehewa vitu vichache." Katika sentensi hii Yesu anaonyesha kanuni za jumla. Hata hivyo, Simon alikuwa anatarajia kuelewa kuwa Yesu anazungumzia kuwa Simoni ameonesha upendo kidogo.

Luke 7:48

Ndipo akamwambia

"ndipo akamwabia mwanamke" (UDB)

Dhambi zako zimesamehewa

"umesamehewa." Hii inaweza ikasemwa katika kauli tendaji NI: "Nasamehe dhambi zako"

kaa pamoja

"kaa pamoja kuzunguka meza" au "kula pamoja"

Nani huyo hata anasamehe dhambi

Viongizi wa dini walijua kwamba Mungu tu anayesamehe dhambi, na hawakuamini kwamba Yesu alikuwa Mungu, Swali hili huenda lilikusudiwa kuwa tuhuma. NI: "Huyu mtu anafikiri kuwa yeye ni nani?" Ni Mungu pekee anaye samehe dhambi!" au "Kwanini huyu mtu anajifanya kuwa Mungu awezaye kusamehe dhambi?"

Imani yako imekuponya wewe

"Kwa sababu ya imani, umeokoka" "imani" inaweza ikatazamwa kama kitendo. NI: "kwa sababu umeamini, umeokoka"

Nenda katika amani

Hii ni namna ya kusema kwaheri wakati huohuo unatoa baraka. NI: "Unapokwenda, usiwe na wasi wasi kabisa" au "Mungu akupe amani unapoenda"

Luke 8

Luka 08 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Kuna nyakati katika maelezo ya sura hii ambapo kuna mabadiliko ya ghafla katika mada. Mtafsiri hapaswi kulainisha mabadiliko haya.

Dhana maalum katika sura hii

Miujiza

Miujiza ya Yesu katika sura hii inaonyesha kwamba alikuwa na mamblaka juu ya mambo yanayozidi udhibiti wa binadamu. Inaonyesha pia kwamba kumwabudu Yesu ni jibu sahihi kwa matendo yake. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#authority)

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Mifano

Mfano ni hadithi fupi inayotumikiwa kwa kuonyesha fundisho ya maadili au wa kidini. Sura hii ina mfano mrefu, unaofunua ukweli kwa wale wanaomwamini Yesu. Pia yanaficha ukweli huo huo kutoka kwa wale wanaomkataa Yesu. Mifano kwa kawaida huchukua fomu ya hadithi.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Kaka na Dada

Sura hii inaanzisha dhana ya kaka na dada "wa kiroho". Maandiko hutumia maneno haya kwa kutaja uhusiano kati ya Waisraeli. Hapa, wale wanaomfuata Yesu sasa wanajulikana kama kaka na dada. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#spirit and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#brother)

<< | >>

Luke 8:1

Taarifa ya jumla:

mistari hii inatoa mrejesho wa habari za Yesu kuhusu kuhubiri wakati anasafiri.

Ilitokea

Hiki kipande cha maneno kimetumika hapa kuweka alama ya sehemu ya habari mpya.

waliokuwa wameponywa na roho wachafu na magonjwa mbalimbali

"Ambao Yesu amewaweka huru kutokana na roho chafu na kuwaponya na magonjwa"

Mary... na wanawake wengi.

"Wanawake watatu waliokuwa wanaitwa: Mariam, Yoana, na Susana.

Yoana, mke Kuza, Meneja wa Herode.

Yoana alikuwa mke wa Kuza, na Kuza alikuja meneja wa Herode. "Yoana, Mke wa meneja wa Herode."

Luke 8:4

Taarifa ya yumla:

Yesu aliwaambia mfano wa mpandaji kwa makutano. Alieleza maana ya ke kwa wanafunzi wake.

Sasa

Hili neno linaonyesha mwanzo wa kitendo katika habari.

mpandaji alienda kupanda mbegu

"mkiulima alienda kupanda baadhi ya mbegu shambani"

zikakanyagwa chini ya miguu

"Zilikanyagwa pia mara zilipoota"

wakazila

"Walizila zote"

Zilipooza

"Miche ikakauka na kupooza"

hazikuwa na unyevunyevu

"ardhi ilikuwa kavu"

Luke 8:7

taarifa unganishi

Yesu anamaliza kuwaambia mfano makutano

zikasongwa

Miti ya miiba ikachukua madini, maji, na mwanga, kwa hiyo miche ya mkulima haikukua vizuri.

zikazaa mazao

"Kuzaa mavuno" au "Kuzaa mbegu zaidi"

Yeyote mwenye masikio ya kusikia na asikie.

inaweza kuwa ni kiasili sana kwa baadhi ya lugha kutumia nafsi ya pili: "Wewe mwenye sikio la kusikia, sikia."

Yeyotemwenye sikio la kusikia

" Anayeweza kusikia" au "Yeyote anayenisikia mimi"

na asikie

"Na asikilize vizuri" au "na awe makini kwa kile ninachokisema"

Luke 8:9

Ujumbe wa kuunganisha

Yesu anaanza kusema kwa wanafunzi wake.

Mmepewa upendeleo wa kujua

"MUngu amewapa ninyi zawadi ya kuelewa" au "Mungu amewafanya watu kuelewa"

siri ya ufalme wa Mungu

Hizi ni kweli kwamba zimejificha lakini Yesu aliwafunulia.

wakiona wasione

"kupitia wanachoona, hawatajua." "kupitia wanavyoona vitu, hawatavielewa" au "kupitia wanavyoona vitu vikitokea, hawataelewa vina maanisha nini."

wakisikia wasielewe

"Kupitia wanavyosikia hawatelewa." "kupitia wanavyosikia maelekezo, hawataelewa ukweli."

Luke 8:11

Ujumbe wa kuunganisha:

Yesu anaaza kuelezea maana ya mfano wa udongo kwa wanafunzi wake.

mwovu shetani hulichukua neno mbali kutoka moyoni

Hii inamaanisha kuwa anawafanya kusahau neno la Mungu ambalo wamelisikia.

hulichukua mbali

Kwenye mfano hii ilikuwa kama fumbo la ndege anayedaka mbegu. jaribu kutumia maneno kwa lugha yako ambayo hutunza picha hii.

kutoka moyoni mwao

Hii ina maana kuwa shetani hukichukua neno mbali mbali na hamu zao za kuliamini neno la Mungu.

ili kwamba wasiamini na kuokolewa

Tangu mwanzo hili lilikuwa kusudi la mwovu, inaweza kutafsiriwa kama. "Kwa sababu mwovu amezama, 'Hawataamini na hawataokolewa"' au "'Hawataweza kuamini kwa matokeo ambayo Mungu atawaokoa."

wakati wa majaribu huanguka

"Wakikutana na magumu wanaanguka mbali na Imani" au "Wanapokutana na magumu wanaacha kuamini"

Luke 8:14

husongwa na huduma na utajiri

"huduma na utajiri na ubora wa maisha huwasonga." "kama palizi huzuia miche mizuri kukua, huduma, utajiri, na ubora wa maisha haya zinawabana hawa watu kukua."

huduma

"vitu ambavyo watu huogopa"

ubora wa maisha haya

"vitu ambavyo kwenye maisha watu hufurahia"

hawazai matunda

"hawazai kuzaa matunda." "kama mche ambao haukui na kuzaa matunda, hawawezi kukua na na kufanya kazi njema."

kuazaa matunda ya uvumilivu

"Kuzaa matunda ya Uvumilivu." Ni kama miche yenye afya inavyozaa matunda mazuri, wanatoa kazi njema kwa uvumilivu"

Luke 8:16

Ujumbe wa kuunganisha:

Yesu aliendelea na mfano mwingine kisha akahitimisha kwa wanafunzi wake kwa kusisitiza jukumu la familia yake katika kazi yake.

Sasa

Hili neno limetumika hapa kuweka alama ya kuanza kwa mfano mwingine.

kinara cha taa

"meza" au "rafu"

hakuna kitakachojificha ambacho hakitajulikana

"kita kitu kilichojificha kitajulikana"

au chochote kilicho sirini ambacho hakitajulikana kikiwa kwenye mwanga

"na kila kitu ambacho ni siri kitajulikana na kuja kwenye mwanga"

unapokuwa unasikiliza

"jinsi gani unasikiliza katika kile ninawaambia" au "Jinsi unavyosikiliza neno la Mungu"

aliye nacho

"yeyote anayesikiliza" au "yeyote anayepokea ninachokifundisha"

kwake ataongezewa zaidi

"vingi atapewa." "Mungu atampa vingi"

asiye nacho

"yeyote ambaye hataaelewa" au "yeyote ambaye hatapokea kile ninachofundisha"

Luke 8:19

Ndugu

Hawa walikuwa wadogo zake Yesu nusu ndugu.

ikaelezwa kwake

"watu wakamwambia" au "mtu fulani akamwambia"

wanahitaji kukuona

"wanasubiri kukuona" au " na wanataka kukuona"

Mama yangu na ndugu zangu ni wale wanaolisikia neno la Mungu na kulitii

"Wale wanaolisikia neno la Mungu na kulitii wanafanana na mam yangu na ndugu zangu kwangu" au "Wale wanaosikia neno la Mungu na kulitii ni mhimu sana kwangu kama mama yangu na ndugu zangu"

Luke 8:22

ujumbe wa kuunganisha

Yesu na wanafunzi wake kisha wakatumia mashua kuvuka ziwa Genasareti. wanafunzi wakajifunza megi kuhusu nguvu ya Yesu kupitia dhoruba iliyotokea.

Sasa ilitokea

Neno hili limetumika hapa kuonyesha alama wa mwanzo wa kipande kipya cha kile kilichotekea.

ziwa

Hili ni ziwa Genesareti ambalo liliitwa ziwa la Galilaya.

walipoanza kuondoka

"walipotoka"

akalala usingizi

"Alilala"

dhoruba kali yenye upepo ikaja

"upepo wenye nguvu ghafla ukaanza kupiga"

Luke 8:24

Bwana mkubwa

Neno la kigriki ambalo limetafsiriwa hapa kama "Bwana mkubwa" siyo neno la kawaida kwa "Bwana mkubwa" hili linahisiana na mtu mwenye mamlaka, na si kwa mtu ambaye anamiliki mtu mwingine. "Bosi" au "Msimamizi" au na neno ambalo linamlenga mtu mwenye mamlaka, kama "Mheshimiwa"

akaukemea

"alizungumza kwa kasi"

vikatulia

"upepo na mawimbi wakakoma"

Imani yenu iko wapi?

Yesu alikuwa anawakemea kwa upole kwa sababu walikuwa hawamwamini kuwa atawajali. "Mlipaswa kuwa na imani" au "Mlipaswa kuniamini"

Huyu ni nani

"Ni mtu wa namna gani huyu."

kwamba anaamuru

Hii inaweza ikawa mwanzo wa sentensi chache: "Anaamuru"

Luke 8:26

ujumbe wa kuunganisha

Yesu na wanafunzi wake wakaja pwani kwa Wagerasi ambapo Yesu aliondoa mapepo mengi kutoka kwa mwanaume.

Mkoa wa Gerasini

Wagerasini walikuwa ni watu kutoka mji ulioitwa Gerasa.

usawa wa Galilaya

"Upande mwingine wa Galilalya"

mtu fulani kutoka mjini

"mtu kutoka mji wa Gerasa"

na huyu mtu alikuwa na nguvu za giza

"mtu ambaye nguvu za giza zilimwendesha" au "huyu mtu alikuwa anaendeshwa na nguvu za giza"

Kwa muda mrefu alikuwa havai nguo.... lakini aliishi kwenye makaburi

Hii ni taarifa ya nyuma kuhusu huyu mtu aliyekuwa na mapepo.

alikuwa havai nguo

"hakuwa anavaa nguo"

Makaburini

Hizi ni sehemu ambazo watu huwa wanaweka miili ya watu waliokufa, yawezekana ni mapango. ukweli kwamba mtu huyu alikuwa anaishi humo inaashiria kuwa haya hayakuwa mashimo yaliyochimbwa chini ya ardhi.

Luke 8:28

Alipomwona Yesu

"yule mwenye pepo alipomwona Yesu"

akalia kwa sauti

"alipiga kelele" au "alipiga yowe"

akaanguka chini mbele yake

"alilala chini ya ardhi mbele ya Yesu." Hakuanguka kwa ajali kama ajali.

kwa sauti kubwa akisema

"Alisema kwa sauti ya juu" au "Alipiga kelele"

Nimefanya nini kwako

"Kwa nini unanitesa mimi"

mwana wa Mungu aliye juu

Hiki ni cheo kikubwa sana kwa ajili ya Yesu.

mara nyingi amepagawa

"mara nyingi walikuwa wanamshika mtu huyu" au "mara nyingi huenda ndani mwake." Hii inatuambia jinsi Pepo alivyofanya mara ya nyingi kabla ya Yesu kukutana naye.

hata kama alikuwa amefungwa.... na kuwekwa chini ya ulinzi

"Hata kama watu walimfunga... na kumbana na kumlinda"

Luke 8:30

Jeshi

imetafsiriwa hii na neno ambalo linahusu kikundi kikubwa cha maaskari au watu. Katika tafsiri zingine zinasema "Legioni." "Kikosi cha" au Brigedia"

twende kwenye shimo

"Kumtoka mtu na kwenda kwenye shimo"

Luke 8:32

Kundi la Nguruwe lilikuwa likichunga juu ya kilima

ona

lilikuwa likichunga juu ya kilima

"lilikuwa karibu linakula majani juu ya kilima"

iyo wale mapepo

Neno "Hivyo" limetumika hapa kuweka alama ya tukio lililotokea kwa sababu ya kitu fulai kingine kilichotokea huko nyuma. kwa jambo hili. Yesu akayaambia mapepo kwamba yaweza kwenda kwa nguruwe.

likakimbia

"Kimbia kwa haraka sana"

Luke 8:34

wakakimbia

"kwa haraka wakakimbia mbali"

wakamwona mtu ambaye mapepo yalikuwa yamemtoka

"walimwona mtu ambaye mapepo yamemtoka"

alikuwa amevaa vizuri

"Alikuwa amevaa nguo"

mwenye akili timamu

"alikuwa na akili timamu" au "alikuwa anaishi kawaida"

amekaa kwenye miguu ya Yesu

"amekaa chini, akimsikiliza Yesu"

na waliogopa

"walimwogopa Yesu"

Luke 8:36

mmoja wao aliyeona kilichotokea

Hawa walikuwa watu waliokuwa na mtu yule wakati Yesu alifanya mapepo yaondoke.

mtu aliyekuwa anaongozwa na mapepo alivyoponywa

Yesu amemwokoa mtu aliyekuwa na mapepo yakimwongoza" au "Yesu alimponya mtu alikuwa na mapepo yakimwongoza"

mkoa wa Gelasini

"Eneo hilo la Gerasini" au "eneo ambapo watu wa wagerasini waliishi"

walikuwa na hofu kuu

"wakajawa na hofu." au "hofu kubwa iliwajaa."

Luke 8:38

Mtu yule

wakati mwingine unapaswa kuaza na hii. "Kabla ya Yesu ana wanafunzi wake kuondoka, yule mtu" au "Kabla ya Yesu na wanafunzi wake hawajawasha mashua yao, mtu"

Nyumba yako

"kaya yako" au "familia yako"

Luke 8:40

Ujumbe wa kuunganisha:

wakati Yesu na wanafunzi wake waliporudi Galilaya upande mwingine wa ziwa, alimponya binti wa mtawala wa sinagogi mwenye miaka 12 na pia mwnamke aliyekuwa akitokwa na damu miaka 12.

taarifa za jumla

Mistari hii inatupa taarifa za nyuma kuhusu Yairo.

makutano wakamkaribisha

"Kwa furaha ya makutano wakamsalimia"

Tazama akaja mtu mmoja anaitwa Yairo

Neno "Tazama" linatutazamisha sis kwa Yairo kama mtu mpya katika habari hii. lugha yako inaweza kukawa na njia nyingine ya kufanya hivi. "Kulikuwa na mtu aliyeitwa Yairo."

mmoja kati ya viongozi katika sinagogi

"mmoja wa viongozi katika sinagogi la mtaa" au "'kiongozi wa watu walikutana kwenye sinagogi katika eneo hilo"

akaanguka miguuni pa Yesu

(1) "Alianguka kwenye miguu ya Yesu" au (2) "alilala chini kwenye ardhi katika miguu ya Yesu." Yairo akuanguka kwa ajali. alifanya vile kama ishara ya ubinadamu na heshima kwa Yesu.

alikuwa katika hali ya kufa

"alikuwa katika hali ya kufa" au "alikuwa karibu na kifo"

Na alipokuwa akienda

Watafsiri wengine wanaweza kusema kwanza, "Hivyo Yesu alikubali kwenda na yule mtu."

makutano walikuwa wakimsukuma dhidi yake

"makutano walikuwa wakijaa kwa kubanana kumzunguka Yesu"

Luke 8:43

mwenye kutokwa damu

"alikuwa anatokwa na damu nyingi" alikuwa akitokwa damu kutoka na tumbo lake hata kama haikuwa kawaida ya wakati wake. kwa kabila baadhi wanaweza wakawa na njia ya upole kuhusiana na hali hii.

hakuna aliyemponya hata mmoja

"lakini hakuna hata mmoja wao wa kumtibu" au "hakuna hata mmoja wao aliweza kumponya"

kugusa pindo la vazi lake

"aligusa pindo la vazi lake" Wanaume wa kiyahudi walivaa Taso juu ya makunjo ya nguo zao kama sehemu ya mavazi ya sherehe zao kama amri katika amri za Mungu. Hii inaonyesha ndiyo alichogusa.

Luke 8:45

Bwana Mkubwa

Neno liliotafsiriwa hapa kama "Bwana mkubwa" siyo neno la kawaida kwa "Bwana mkubwa." Hii inaenda kwa mtu mwenye mamlaka, lakini si kwa mtu mwingine yeyote. "Bosi" au "Msimamizi" au na neno ambalo ni la kawaida limetumika kuelezea mtu aliye kwenye mamlaka, kama vile "Mheshimiwa"

umati wa watu wanakusukuma na wanakusonga

Kwa kusema hiv, Petro alikuwa akihusisha kila mmoja anaweza kumgusa Yesu. hii ni taarifa thabiti inaweza kufanywa kwa wazi kama ni mhimu katika UDB

nilijua nguvu zimetoka kwangu

"Nimesikia uponyaji nguvu zimetoka kwangu." Yesu hakupotwza nguvu au kuwa mdhaifu, lakini nguvu yake inamponya mwanamke.

Luke 8:47

hawezi kuficha alichokifanya

"hawezi kutunza siri ya kile alichokifanya." "kwamba asingeweza kuendelea kutunza kama siri maana yeye ni yule aliyemgusa Yesu."

akaanza kutetemeka

"akatetemeka kwa hofu"

akaanguka chini mbele za Yesu

yawezekana maana ni 1). "aliinama chini mbele za Yesu" au 2) alilala chini kweye ardhi katika miguu ya Yesu. "hakuanguka kiajali. alifanya hivi kama ishara ya ubinadamu na heshima kwa ajili ya Yesu.

mbele ya

"Kwenye sehemu ya" au "Mbele"

Binti

Hii ilikuwa ni aina ya kusema kwa mwanamke. Kabila lako linaweza kuwa na njia nyingine ya kuonyesha huu wema.

imani yako imekufanya uwe vizuri

"Kwa sababu ya Imani yako, umekuwa vizuri." "Kwa sababu umeamini, umeponywa"

Enenda kwa Amani

Hii ni njia ya kusema, ""Kwa heri" na kutoa baraka kwa wakati mmoja. "Unapokwenda, Usiogope hata kidogo" au "Mungu akupe amani unapoenda"

Luke 8:49

Alipokuwa akiendelea kusema

"wakati Yesu alipokuwa akiongea kwa mwanamke"

kiongozi wa sinagogi

Hii inarudi kwa Yairo.

alimjibu

"Yesu alimjibu Yairo"

ataokolewa

"Nitamponya"

Luke 8:51

Kisha alipokuja kwenye nyumba

"Kisha walipokuja katika nyumba, Yesu"

isipokuwa Petro, Yohana na Yakobo, baba yake binti, na mama yake

"aliwaruhusu Petro, Yohana, Yakobo, baba yake binti, na mama yake kuingia ndani"

watu wote walikuwa wanaomboleza na kutoa sauti kwa ajili yake

"watu wote walikuwa wanaonyesha huzuni zao na kulia kwa sauti kwa sababu binti amekufa"

Luke 8:54

Mtoto, inuka

"Binti mdogo, amka"

roho yake ikarudi

"akawa mzima" au "akawa hai tena"

roho

"pumzi" au "Uhai"

Luke 9

Luka 09 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

"Kuhubiri ufalme wa Mungu"

Kuna mzozo kati ya wasomi kuhusu maana ya ufalme we Mungu hapa unamaanisha utawala wa Mungu duniani au ujumbe wa injili (Yesu alikufa kwa ajili ya dhambi za mwanadamu). Ni bora kutafsiri hii kama "kuhubiri juu ya ufalme wa Mungu" au "kuwafundisha kuhusu jinsi Mungu angeweza kujionyesha kuwa mfalme." "Ni bora usitafsiri maneno hayo kama mfano wa injili kwa sababu haifai hapa. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

Eliya

Nabii Malaki alitabiri kwamba siku moja Eliya angerudi kabla Masihi hajaja. Yesu anaelezea kwamba Yohana Mbatizaji alitimiza unabii huu kwa kumtumikia Mungu kwa namna ileile kama Eliya. Eliya ametajwa kwa njia mbili tofauti katika sura hii, kama mtu halisi na kurudi kimfano kwa Eliya. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#prophet and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#christ)

"Ufalme wa Mungu"

Maneno 'ufalme wa Mungu' katika sura hii yalitumikiwa kwa kutaja ufalme utakapokuja wakati maneno haya yaliyosemwa. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#kingdomofgod)

"Waliona utukufu [wa Yesu]"

Katika Maandiko utukufu wa Mungu unaonekana kama mwanga wa kunga'a sana. Utukufu wa Mungu Katika Maandiko utukufu wa Mungu unaonekana kama mwanga wa kunga'a sana kwa mtu anayeuona. Tukio hilo, iliyoandikwa katika sura hii, linaitwa "kugeuka sura," asababu Yesu aligeuka sura na kubadilika sura ili aonyeshe utukufu wake wa kiungu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#glory and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#fear)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Kitendawili

Kitendawili ni taarifa inayoonekana kuwa ya ajabu, ambayo ni kana kwamba inajikana yenyewe, lakini kwa hakika sio ya ajabu. Mfano wa kitendawili katika sura hii: "Yeyote anayetaka kuokoa maisha yake ataipoteza, na yeyote anayepoteza maisha yake kwa ajili yangu ataipata." (Luka 9:24).

"Mwana wa Binadamu"

Yesu anajiita mwenyewe kama "Mwana wa Binadamu." Lugha zingine haziwezi kuruhusu mtu kujitaja mwenyewe kama 'mtu wa tatu.' (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sonofman)

"Kupokea"

ULB inatumia neno hili mara kadhaa katika sura hii kwa maana mbalimbali. Yesu anasema, "Yeyote akipokea mtoto mdogo kama huyu kwa jina langu, yeye ananipokea pia, na yeyote akinipokea mimi, anapokea pia yeye aliyenituma" (Luka 9:48). Katika aya hii, "kupokea" inaweza kutafsiriwa kama "kutumikia." Katika mstari mwingine inasemwa, "watu huko hawakumpokea" (Luka 9:53). Katika aya hii, "kupokea" inaweza kutafsiriwa kama "kuamini" au "kukubali." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#believe)

<< | >>

Luke 9:1

Sentensi Unganishi

Yesu anawakumbusha wanafunzi wake waasitegemee pesa na vitu nyao, anawapa nguvu, na pia awatuma waende sehemu mbalimbali.

nguvu na mamlaka

Maneno haya mawili yametumika pamoja kuonesha kwamba wale kumi na wawili walikuwa na uwezo na haki ya kuponya watu.

magonjwa

"ugonjwa"

aliwatuma nje

"aliwatuma sehemu mbalimnbali" au "aliwambia waende"

Luke 9:3

Akawaambia

"Yesu akawaambia wale thenashara"

Usichukue chochote

AT." usichukue chochote" au "usije na chochote"

Kwaajili ya safari yako

"kwa ajili ya safari yako" au "wakati unasafiri." Wasichukue chochote kwaajili ya safiri yao yote, watapita kijiji kwa kijiji mpaka warudi kwa yesu.

fimbo

"fimbo" au "fimbo ya kutembelea." ilikuwa ni fimbo kubwa iliyotumika kumsaidia mtu wakati wa kupanda au kwenye barabara mbovu. ilikuwa ikitumika pia kujilinda dhidi ya watekaji.

Mkoba

ni mfano wa kibebeo(begi) ambalo wasafiri hutumia kwa kubebea kile anachokitaka safarini.

Mkate

AT: "Chakula"

Nyumba yeyote mtakayoingia

"Nyumba yoyote mtakayoingia"

Kaeni humo

"Bakieni humo" au "muishi kwa mda ndani ya ile nyumba kama wageni"

Kutoka mahali hapo

"kutoka mjini" au "kutoka katika sehemu ile"

Luke 9:5

Na kwa wale watakao kataa kuwapokea

AT: " hiki ndo mtakachofanya kwa watu watakao kataa kuwapokea"

mtakapo ondoka

"waliondoka sehemu ambayo yesu alikuwepo"

kila mahali

"walienda kila mahali"

Luke 9:7

Taarifa kamili

Mistarin hii inapingan kutoa taarifa kuhusu Herode

sasa

hili neno limetumika kuonesha pumziko katika story kamili. Hapa Luka anasimulia taarifa za msingi za Herode.

Herode, mkuu wa mkoa

Inamwakilisha Herod ambae alikuwamtawala wa moja ya nne ya Israel.

alitaabika sana

"alikasirika sana" au "alikuwa anashangaa"

Nilimkata kichwa Yohana

AT: "niliwaamlisha wanajeshi wangu wamkate kichwa Yohana"

Luke 9:10

Sentensi unganishi

Ingawa wafuasi walirudi kwea yesu na wakaenda Bethadia kupumzika, makutano walimfata yesu awaponye na kusikiliza mafundisho yake. Aliwasaidia kugawanyisha mkate na samaki wakati wanarudi nyumbani.

wale waliotiumwa

AT: " wale mitume kumi na mbili aliowatuma yesu"

walirudi

"walirudi pale alipokuwa yesu"

wakamuambia

"mitume wakamuambia yesu"

kila kitu walichofanya

Hii ina wakilisha mafundisho na uponyaji waliofanya walipoenda kwenye miji.

aliwachukua , aliondoka mwenyewe

Yesu na mitume wake waliondoka wenyewe. AT: "aliwachukua wakaondoka pamoja"

Bethadia

Hili ni jina la mji.

Luke 9:12

Siku ikaanza kuisha

"jua lilivyoanza kuzama" au " siku ilivyoanza kuisha"

Watawanye makutano

"kuwaambia makutano waondoke"

labda twende tukanunua chakula

AT: " labda tutaenda kununa chakula" au " labda kama twende kununua chakula" au unaweza kuanza sentyensi mpya "kama wewe unataka tuwalishe, tutatakiwa kwenda kununua chakula."

kama wanaume elfu tano

"kama wanaume elfu tano." hii number haijumuishi wanwake na watoto ambao yaweza kuwa walikuwepo.

wakalisheni

"waambieni wakae"

"hamsini kila "

"50 kila "

Luke 9:15

Wakafanya hivyo

wanfunzi wakawakalisha makutano kwenye makundi ya watu hamsini hamsini.

akachukua

"yesu akachukua"

mkate

kiwango maarumu cha mkate wa kuokwa. AT: "mkate mzima"

na akiangalia

"wakati anaangalia" au " baada ya kuangalia"

juu mbinguni

Hii inawakilisha kuangalia juu, kuelekea mawinguni. Wayahudi waliamini kuwa mbingu iko juu mawinguni.

watenge mbele ya

"kuwagawia" au " kuwapa"

wakashiba

AT: "walikula kama walivyotaka"

Luke 9:18

Sentesi kiunganishi:

Yesu akisali, pekee yake na wanfunzi wake, na kuanza kuongelea kuhusu yesu ni nani. Yesu anawaambia kuhus kifo chake na ufufuo utakao fata na kuwataka wamfate yeye hata iweje.

Nayo ikawa kwamba

Hii sentensi inaashiria mwanzo wa tukio jipya.

alipokuwa akiomba

"yesu alipokuwa akiomba"

kusali pekee

Wanfunzi walikuwa na yesu, lakini alikuwa anasali pekee yake na yeye mwenyewe kwa siri.

kujibu, wakasema

"walimjibu wakisema"

Yohana mbatizaji

AT: "wengine wanasema wewe ni Yohana mbatizaji"

kutoka nyakati za zamani

"ambae aliishi muda mrefu uliopita"

amefufuka tena

"alifufuka"

Luke 9:20

Akawaambia

"yesu akawaambia wanafunzi wake"

kujibu, Petro akasema

"Petro alijibu na kusema" au "Petro alijibu kwa kusema"

Lakini kwa kuwaonya, Yesu akawaelekeza

AT: "Lakini yesu waliwaonya na kuwaelekeza" au '"Ndipo yesu waliwapa onyo kali"

kutomwambia yoyote

"kutokumwambia mtu yoyote" au " wasimwambie mtu yoyote." Hii inaashiria msemo. AT: "lakini kuwaaonya, yesu aliwaambia, "msimwambie mtu yoyote"

kwamba mwana wa Adamu atateseka kwa vingi

AT: "kwamba watu wanweza msababishia mwana wa Adamu kuteseka sana." Hii pia inaweza kutafasiriwa kama msemo wa moja kwa moja kwa sababu ipo kwenye UBS.

na kukataliwa na wazee na wakuu wa Makuhani na waandishi

AT: "na wazee, wakuu wa makuhani, na waandishi watamkataa"

na atauliwa

AT: " na watu watamuua"

kwenye siku ya tatu

"siku tatu baada ya kufa" au "kwenye siku ya taut baada ya kifo chake"

atafufuka

"atawekwa hai." AT: "Mungu atamfanya hai tena" au "atafufuka"

Luke 9:23

akawambia

yesu akawaambia

wote

Hii inamaanisha wanafunzi wake wote waliokuwa na yesu.

kunifata mimi

"kunifata mimi" au "kuongozana na mimi kama mwanafunzi"

ajikane

AT: "kujijitoa kwa nfasi yake mwenywe," au "na aache tamaa yake mwenyewe"

achukue msalaba wake kila siku

"auchukue na aubebe msalaba wake kila siku." Hii haimaanishi aubebe msalaba kila siku. Inamaanisha wafuasi wake wakatae vitu wanavyovitakana wawe tayari kuteseka na kufa ili kumtii yesu.

anifuate

"kenda pamoja na mimi" au "kuanza kunifuata na kuendelea kunifuata"

kitamfaidia nini mwanadamu...binafsi?

Yesu anatumia swali kuwafundisha wanafunzi wake. AT: "mwanadamu hapati kitu chochote kizuri...binafsi."

kama akiupata ulimwengu wote

"kama atapata kila kitu ulimwenguni"

akapoteza au akapata hasara yake binafsi

AT: "yeye mwenyewe atapotea"

Luke 9:26

na maneno yangu

AT: "na nilichosema" au "na nilichofundisha"

yeye mwana wa Adam atamuonea aibu

"mwana wa Adam atamuonea aibu"

mwana wa Adam

Yesu alikuwa anajiongelea yeye mwenyewe. AT: "mimi, mwana wa Adam"

atakapo kuwa katika utukufu wake

Yesu anajiongelea yeye mwenyewe kupitia nafsi ya tatu. AT: "nitakapokuja kwenye utukufu wangu"

baadhi yenu wasimamao hapa

"baadhi yenu mliosimama na mimi hapa"

hawata ionja mauti mpaka wauone ufalme wa Mungu

AT: "watauona ufalme wa Mungu kabla hawajafa" au "utauona ufalme wa Mungu kabla huja"

Luke 9:28

Sentensi kiunganishi

Siku nane baada ya Yesu kuwaambia kuwa baadhi hawatakufa kabla ya kuuona ufalme wa Mungu, Yese anaenda mlimani kuomba pamoja na Petro na Yohana ambao walilala wakati Yesu anabadilika muonekano .

Ikatokea

Hii sentenso imetumika hapa kuashiria tukio muhimu katika hadithi. Kama lugha yako ina namna nzuri ya kufanya hivi, unaweza kufikria kuitumia hapo.

siku nane

"siku 8"

maneno haya

Hii inaashiria Yesu alisema kwa wanafunzi wake kwenye mistari inayoendelea.

juu ya mlima

Haiko wazi ni juu kiasi gani walienda. AT: "pembeni mwa mlima"

meupe na ya kung'aa

"nyeupe ya kungaa na kali" au "nyeupe kali na ya kungaa"

Luke 9:30

Tazama, walikuwepo wanaume wawili wanaongea

Neno "tazama" hapa liaashiria tuwe makini kwa taarifa ya kushangaza inayofata. AT: "ghafla kulikuwa na wanaume wawili wanaongea" au "ghafla wanaume wawili walikuwa wanaongea."

walionekana katika utukufu

Hii sentensi ya kuoanaisha inatoa taarifa kuhusu Musa na Elisha. AT: "na walionekana wenye utukufu"

kuondoka kwake

"kuondoka kwake" au "atakavyooondoka." AT: "kifo chake."

Luke 9:32

sasa

Hii sentensi ya imetumika kuashiria pumziko kwenye hadithi wenyewe inayotolewa, Hapa Luka anasimuili taarifa kuhusu Musa na Yakobo, na Yohana.

waliuona utukufu wake

Hii inamaanisha mwanga uliowaka kuwazunguka. AT: "Aliona mwanga mkali unawaka kwa yesu" au "waliona mwanga mkali unatokea ndani ya Yesu"

wanaume waili walikuwa wamesimama nae

Inamaanisha Musa na Elisha.

Ikatokea kwamba

Hii sentensi imetumika hapa kuonesha matukio yananza. Kama lugha yako ina maana nzuri zaidi , unaweza fikiria kuitumia hapa.

Bwana

Neno lililotafasiriwa hapa kama "Bwana" sio neno la kwawaida kumaanisha " Bwana." Hili linamaanisha mtu mwenye mamlaka na sio mtu anaemmiliki mtu mwingine. AT: "Bosi"au "kiongozi" au neno huwa linatumika kueleza mtu mwenye mamlaka, mfano kama "Sir"

malazi

"hema" au "kibanda"

Luke 9:34

Alipokuwa akisema vitu hivi

"Wakati Petro alikuwa akisema viotu hivi"

waliogopa

Hawa wanafunzi wazima hawakuogopa mawingu. Msitari unaashiria woga usio wa kawaida ulitokea juu yao kupitia mawing. AT: "walishitushwa"

walivyokuwa wamezungukwa na wingu

AT: "kama mawingu yalivyo wazunguka"

Sauti ikatoka winguni, ikisema

AT: "Mungu akaongea nao kupitia mawinguni akisema"

mwanangu uliyechaguliwa

Neno "kuchaguliwa" linatoa taarifa kuhusu mtoto wa Mungu. Haisemi kuwa Mungu alikuwa na mtoto zaidi ya mmoja. AT: "mwanangu niliuyekuchagua" (UDB) au "mwanangu,uliyechaguliwa"

walikaa kimya, na katika siku hizo... vitu walivyoona

Hii ni taarifa inayosema kilichotokea baada ya hadithi kama matokeo ya hadithi yenyewe.

siku hizo

Hizi zinaweza kuwakirisha siku ambazo mpaka Yesu anachukuliwa mawinguni baada ya ufufuo au yaweza kuwa baada ya siku ambazo Yesu alitoa kauli.

Luke 9:37

Sentensi unganishi

Siku ya pili baada ya Yesu kubali muonekano, Yesu alitoa pepo lililokuwa limemuingia kijana ambae wanafunzi walishindwa kumponya.

Ikatokea

Hii tungo inaashiria mwanzo wa sehemu nyingine ya hadithi, Kama lugha yako ina maana nzuri zaidi , unaweza fikiria kuitumia hapa.

Tazama, mwanaume kutoka kwenye kusanyiko

Neno "tazama" linatujulisha juu ya mtu mpya anaetokea kwenye hadithi. lugha yako ina maana nzuri zaidi. Kiingereza kinatumia "kulikuwa na mwanaume kwenye kusanyikao"

unaona, roho

Tungo "unaona" inatutambulisha kwa pepo kwenye hadithi ya mwanadamu. lugha yako ina maana nzuri zaidi. Kiingereza kinatumia "kulikuwa na pepo"

Lilitoka kwa tabu

inaweza kuwa na maana hizi 1) "vigumu kumuacha kamwe mwanangu" (UDB) au 2) "ni ngumu kwa mwanangu wakati linatoka"

povu mdomoni

Wakati mtu anamshituko, wanaweza kupata shida kupimua au kumeza. Hii inasababisha povu jeupe kutokea kwenye midomo yao. Kama lugha yako inaweza elezea vizuri, itumie.

Luke 9:41

Yesu akajibu akasema

"kwenye jibu Yesu akasema"

Enyi kizazi kisicho amini na wachafu

Hii ilielezwa kwenye umati uliokuwa limekusanyika, na sio kwa wanafunzi.

mpaka lini nitazidi kuwabeba

Hapa "nita" ni wingi. Yesu anatumia swali kukemea umati. AT: "nimefanya merngi na bado hamuamini!"

Mlete mwanao hapa

Hapa "wako" ni umoja. Yesu snaongea moja kwa moja na baba wa anaemshughulikia.

aliokuwa anakuja

"anakuja" au "yuko anakuja"

aliikemea

"alizungumza kwa ukali kwa"

Luke 9:43

Wote walishangazwa kwa ukuu wa Mungu

Yesu alifanya miujiza , lakini umati haukutambua nguvu za Mungu zilitumika kuponya.

aliyo yafanya

"kwamba Yesu alifanya"

Maneno haya yazame kwa undani masikioni mwenu

AT: "sikizia kwa makini na ukumbuke" au "usisahau hili"

kwa kuwa mwana wa Adamu atatolewa kwenye mikoni ya wanadamu

Hapa " mikono" inamaanisha nguvu au utawala. AT : "wanadamu watamkabidhisha mwan wa Adamu kwenye mamlaka."

mwana wa Adamu

Yesu anajiongelea mwenyewe kwenye nafsi ya tatu. AT: "mimi, mwana wa Adamu"

Lakni hawakuelewa maana ya neno hili

AT: "wahakujua anaongelea kifo chake"

na lilifichwa juu yao

AT: "Mungu aliwafichia maana yake"

Luke 9:46

Taarifa kamili

Mzozo kuhusu madarsks ukanza kati ya wanafunzi.

kati yao

"kati ya wanafunzi"

wakihojiana mioyoni mwao

AT: "kufikiria juu ya mtu mmoja mmoja" au "kufikilia kimoyoni"

jina langu

Hii inawakilisha mtu anaefanya jambo au an kama muwakirishi wa Yesu. AT: "kwa sababu yangu

anampokea pia

AT: "ni kama amenipokea mimi"

aliyenituma mimi

"Mungu, aliyenituma"

Luke 9:49

Petro akajibu akasema

Yohana alikuwa anajibu juu ya kile Yesu alichosema kuhusu ukuu. Hakuwa anajibu swali. alitaka kujua mtu aliye yalhimiza mapepo kutoka atakuwa na nafasi gani kati ya wanafunzi. AT : "kwenye kujibu, Yohana akasema" au "Yohana alijibu kwa Yesu"

Bwana

Neno lililotafasiriwa hapa kama "Bwana" sio neno la kwawaida kumaanisha " Bwana." Hapa linamaanisha mtu mwenye mamlaka na sio mtu anaemmiliki mtu mwingine. AT: "Bosi"au "mweshimiwa"

jina lako

Hii inamaanisha mtualiyekuwa anaongea alikuwa na nguvu na mamlaka ya Yesu.

Msimzuie

AT: "mruhusu aendelee"

kwa kuwa asiye kinyume na ninyi ni wa kwenu

Baadhi ya lugha ina misemo inayomaanisha kitu kile kile. AT: "kama mtu asipokuzuia , ni kama anakusaidia" au "kama mtu hatendi kinyume na wewe, anafanya sawa sawa na matakwa yako."

Luke 9:51

Taarifa kwa ujumla

Na sas ni dhahili kuwa Yesu ameamua kwenda Yerusalem.

Ikatokea kwamba

Hii tungo imetumika hapa kuashiri mwanzo wa sehemu mpya ya hadithi

siku zake za kwenda juu zilikaribia

"muda ulikuwa unafika wa yeye kwenda juu" au " muda ulikaribia wa yeye kwenda juu"

aliazimia

"kudhamilia" au "kukusudia"

weka uso wake

AT: "alifikiria akilini mwake" au "aliamua"

kumuandalia

Hii inamaanisha kufanya mipango ya kufika katika eneo, inawezekana kuunganisha eneo la kuongealea, anaeo la kukaa, na chakula.

Hawakumpokea

"hawakumkaribisha" au au hawakutaka abaki"

Luke 9:54

liona hili

"aliona kwamba wasamaria hawakumpokea Yesu"

tuamuru moto ushuke chini kutoka mbinguni uwateketeze

Yakobo na Yohana walipendekeza njia hii ya hukumu kwa sababu walijua kwamba hivi ndivyo manabii kama Elia walivyo hukumu watu waliomkataa Mungu.

aliwageukia akawakemea

"Yesu aligeuka na kuwakemea Yakobo na Yohana." Yesu hakuwahukumu Wasamaria , kama wanafunzi walivyo tegemea.

Luke 9:57

mtu mmoja

Huyu hakuwa moja ya wanafunzi

Mbweha wanamashimo

Yesu anajibu kwa mithali ili kufundisha watu kuhusu kuwa mwanafunzi wa Yesu. Yesu anajibu kwamba kama mtu atahitaji kumfuata, kwamba mtu huyo anaweza asiwe na nyumba. AT: "Mbeha wana mashimo...wala sehemu ya kulaza kichwa. Hivyo usitegemee kama utakuwa na nyumba"

Mbweha

Hawa ni wanyama wa nchi sawa na mbwa. Wanalala katika mapango au shimo katika arthi.

ndege wa angani

"ndege wanaoruka angani"

mwana wa Adamu

"Yesu anaongea kuhusu yeye mwenyewe katika nafsi ya tatu"

hana pakulaza kichwa chake

"sina sehemu ya kulaza kichwa changu" or "wala sehemu ya kulala." Yesu anakuza ili kujenga hoja kwambaalikuwa hakalibishwi popote kuishi.

Luke 9:59

Sentensi Unganishi

Yesu anaendelea kuongea na wanafunzi wake akiwa pembezoni mwa barabara.

Mnifuate mimi.

Hii ina maanisha kuwa mfuasi wa Yesu na kwenda pamoja naye.

Mniruhusu kwanza niondoke

"Kabla sijafanya hivyo, mniache niende."

Waache wafu wawazike wafu wa kwao

Kwa sababu watu waliokwisha kufa hawawezi kumzika mtu yeyote, Maana inayokusudiwa hapa ni ya kwamba watu walio wafu katika roho wawazike watu walio wafu katika mwili.

Luke 9:61

Nitakufata

"nitaungana nawe kama mwanafynzi" au " niko tayari kukufata"

kwanza ni ruhusu nikuagae

"kabla sijafanya hivyo, niruhusu niseme kwaheri" au "niruhusu kwanza niwaambie naondoka"

walio katika nyumba yangu

"nyumba yangu" au "watu wa nyumabani kwangu"

Hakuna anaefaa kwa ajili ya ufalme wa Mungu

Yesu anajibu mithari kumfundisha mwandamu kwa mwanafunzi wake, Yesu anamaanisha mtu hafai kwa ajili ya ufalme wa Mungu kama anafata watu wa nyuma badala ya kumfata Yesu

"Atiae mkono wake kwenye jembe

AT: " baada ya kuanza kulima shamba lake" au "baada ya kuanza kuandaa shamba lake"

akaangalia nyuma

Mtu anaangalia nyuma wakati analima hawezi kuliongoza vizuri jembe pale linapotakiwa kwenda. Wanatakiwa kuwa makini kuangalia mbele ili walime vizuri.

kufaa kwa

"kufaa kwa" au " kizuri kwaajili ya"

Luke 10

Luka 10 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Mavuno

Mavuno ni picha ya kawaida inayotumiwa katika Agano Jipya. Wakati watu wanakuja kwa Yesu na kumwamini inajulikana kama mavuno. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith)

"Alikuwa jirani"

Dhana ya "kuwa jirani" ilikuwa muhimu katika desturi ya inchi za kale za Mashariki ya Karibu, ambayo kukaribisha wageni ilikuwa heshimu sana. Katika sura hii, "jirani ina maana ya mtu anayesihi karibu au labda mtu mwingine ye yote. "Alikuwa jirani" pia hutumiwa kumaanisha "alikuwa jirani mwema."

<< | >>

Luke 10:1

Taarifa kwa ujumla

Yesu anawatuma zaidi ya watu sabini mbele yake. Hao sabini wanarudi na furaha , na Yesu anawajibu kwa kumuabudu baba wa mbinguni.

sasa

Neno hili limetumika kuashiria tukio jipya katika hadithi.

sabini

"70." matoleo mengine yanasema "sabini na mbili" au "72." utatakiwa kuweka maezezo yanayosema ivyo.

Aliwatuma huko, wawili wawili

"Aliwatuma huko katika makundi ya wawili wawili" au "Aliwatuma huko wawili wawili katika kila kundi"

Akawaambia

Hii iikuwa kabla hawajaondoka. AT: "Hiki ndo alichowaambia" au "kabla hajaondok aliwaambia."

Mavuno ni mengi, lakini wafanyakazi ni wachache

"kulikuwa kuna mazao mengi, lakini

Luke 10:3

enendeni katika njia zenu

"enendeni kwenye majiji" au "enendeni kwa watu"

ninawatuma nje kama kondoo katikati ya mbwa mwitu

Hii inamaana ya kuwa kuna watu wangewadhuru wale ambao Yesu aliwatuma. Majina ya wanyama wengine yangeweza kuwakilishwa. AT;"Nitakapowatuma huko nje watu watawadhuru kama ambavyo mbwa mwitu huwaingilia kondoo"

Mbwa mwitu

Hii imetafasiriwa na maana halisi ya "mbwa wa mwituni" au "mbwa wakali" au jina la mnyama wa pekee kama mbwa ambaye watu huwa wanamfaham.

Musibebe mfuko/mikoba yenye pesa.

"Musichukue Mikoba yenye pesa ndani yake"

Msimusalimie yeyote muwapo njiani.

Yesu alikuwa anasisitiza ya kuwa waende kwa haraka huko mjini na wafanye hii kazi. Hakuwambia wawe wakorofi au watu wabaya.

Luke 10:5

Amani iwe katika nyumba hii

Hii ilikuwa ni salamu na baraka. Hapa "nyumba" inawakilisha watu wanaoishi ndani ya nyumba. AT: "watu wa nyumba hii na wapokee amani."

mtu wa amani

"mtu mwenye amani." Huyu ni mtu anaetaka kuwa na amani na Mungu na watu.

amani yenu itabaki juu yake

AT: "atakuwa na amani aliyombarikia"

kama sivyo

AT: "kama hakuna mtu mwenye amani huko" au "mwenye nyumba sio mtu wa amani"

itarudi kwenu

"hatokuwa na hiyo amani" au "hatoipokea hiyo amani uliyombarikia"

Mbakie katika nyumba ile ile.

Yesu hakumaanisha waendelee kubakia ndani ya nyumba kwa siku nzima, ila wapate kulala katika nyumba mojakila usiku. AT:" Kuendelea kulala katika nyumba"

Mfanya kazi anasitahili mshahara wake

Yesu alikuwa alikuwa akizungumzia wale watu aliowatuma huko nje. Kwa sababu wangekuwa wakiwafundisha na kuwaponya watu, hivyo watu wangewapatia mahali pa kukaa pamoja na chakula.

Msiende nyumba kwa nyumba

AT:" Msilale sehemu/nyumba tofauti tofauti katika kila usiku"

Luke 10:8

Na wakawapokea ninyi.

" Kama wakiwakaribisha"

Kuleni chochote kitakachowekwa mbele yenu

AT " kuleni chakula chochote watakacho wapeni"

Ufalme wa Mungu umekaribia kwenu,

Hii inarejea ya kuwa kazi ya ufalme wa Mungu ilikuwa ikifanyika mahali pale kupitia uponyaji kwa wanafunzi wake na mafundisho ya Yesu. AT:" Munaweza kuuona ufalme wa Mungu ukiwazunguka ninyi".

Luke 10:10

Na wasiwapokee

"kama wakiwakataa"

Hata vumbi lililonatia miguu yetu kutoka katika mji wenu tunalikung'uta thidi yenu

Kwa sababu Yesu alikuwa akiwatuma watu hawa huko nje katika makundi ya watu wawili wawili, hivyo watu wawili wawili walikuwa wasemaji kwa kila kundi. kwa hiyo lugha zenye tafasiri ya neno "sisi" ndo ilikuwa hivyo. AT: "Kama ambavyo mlitukana sisi, na ndivyo tutakavyo wakana ninyi. Na hata tumekataa vumbi linalo toka katika mji wenu linalonata katika miguu yetu".

Lakini tambueni hili, Ufalme wa Mungu umekaribia.

Neno "Lakini tambueni hiii" linatambulisha onyo. Linamaanisha "hata kama mkitukana sisi, haibadilishi maana ya ufalme wa Mungu kuwepo hapa".

Ufalme wa Mungu umekaribia.

"Ufalme wa Mungu upo kati yenu"

Ninasema kwenu

Yesu alikuwa akiyasema haya kwa watu sabini(70) ambao alikuwa akiwatuma huko nje, Alisema haya ili kuonesha ya kuwa alikuwa aseme kitu cha muhimu zaidi"

Siku ya hukumu

kwa kawaida neno linasema "siku ile"Lakini wanafunzi wake walielewa ya kuwa, alimanisha siku ya mwisho ya hukumu kwa wenye dhambi.

Itakuwa ni usitahamilivu zaidi kwa Sodoma kuliko mji huo.

"Mungu hataihukumu Sodoma kwa nguvu kama atakavyouhukumu ule mji" AT "Mungu atawahukumu watu wa ule mji kwa nguvu zaidi ya atakavyo wahukumu watu wa Sodoma".

Luke 10:13

Ole kwako Korazini, Ole kwako Bethadia!

Yesu aliongea kana kwamba watu wa Korazini na Bethadai walikuwepo, lakini hawakuwepo.

Kama kazi kuu zilizo fanyika ndani yako ingali fanyika Tire na Sidoni.

Yesu anaelezea hali ambayo ingetokea hapo nyuma lakini haikutokea. AT: " Kama mtu angelitenda miujiza kwa watu wa Tire na Sidoni ambayo ningetenda kwenu"

Wangeli tubu zamani sana,

"Watu wanyonge walioishi huko wangelionesha huzuni ya dhambi zao".

wakikaa ndani ya nguo za gunia na majivu.

"Wakivaa nguo za magunia na kukaa kwenye majivu"

Lakini itakuwa usitahamilivu zaidi siku ya hukumu kwa Tire na Sidoni zaidi yenu.

AT: "Lakini kwa sababu hamkutubu na kuniamini mimi hata kama mliniona nikitenda miujiza, Mungu atawaadhibu zaidi ya jinsi ambavyo atawadhibu Tire na Sidoni"

Katika hukumu

"Siku ya mwisho ambapo amaungu atamuhukumu kila mmoja.

Wewe Kaperanaum,

Yesu anaongea na watu wa mji wa Kaperanaum, kama vile walikuwa wakisikiliza kumbe ndivyo sivyo.

Unafikiri utainuliwa mpaka Mbinguni?

Yesu anatumia swali kuwakalipia watu wa Kaperanaum kwa kujisifu kwao. AT : "Hautakaamufikie juu mpka mbinguni" au "Mungu hatakuheshimu"

Utashushwa chini mpaka kuzimu

AT: "Utaenda chini kuzimu" au " Mungu atakupeleka kuzimu".

Luke 10:16

Atakaye wasikiliza ninyi anisikiliza mimi

AT: "Mtu akiwasikiliza, ni kama ananisikiliza mimi"

Yeyote awakataapo anikataa mim

"Atakaye wakataa ninyi, amenikataa mimi".

Yeyote anikataaye mimi amtakaa aliyenituma"

Atakaye nikataa mimi, itakuwa kama anamkataa yeye aliyenituma".

Aliyenituma mimi.

Hii inarejea Mungu Baba aliemuteuwa Yesu kwa ajili ya kazi Maalumu. AT: " Mungu, alienituma".

Luke 10:17

Wale sabini walirudi

Lugha zingine zinaweza sema ya kuwa wale sabini walienda kwanza huko nje kama ambavyo UDB inasema. Hii ni taarifa ya mwanzo inayoweza fanya ya mwisho.

Sabini

Unawezataka kuongeza idadi, kwa maana ya kwamba, "Andishi mbalimbali wana 72 badala ya 70.

Katika jina lako

kwa hapa, "Jina" lina rejea Nguvu na mamulaka ya Yesu".

Nilimtazanma Shetani akianguka kutoka mbinguni kama radi.

Yesu alitumia mfano hai, kuonesha jinsi ambavyo Mungu alikuwa akimshinda shetani pale ambapo wanafunzi wake 70 walikuwa wakihubiri mjini".

Mamlaka ya kukanyaga nyoka na nge

"Mamlaka ya kukanyaga nyoka na kusaga n'ge" Maana zinazotambulika ni kama, 1)Hii inarejea uhalisia wa nyoka na n'ge. au 2) Nyoka na nge ni vielelezi wa roho chafu. UDB inatoa tafasiri ya kuwa hizi ni roho chafu. "Nimewapa haki na mamlaka ya kuteka roho chafu"

Mamlaka juu ya pepo wabaya na n'ge

Hii inamaana ya kuwa watafanya haya na hawatadhurika. AT:Watatembea juu ya nyoka na n'ge na hawatawadhuru".

N'ge

Mnyama mdogo mwenye sehemu mbili za kushikia mfano wa pembe, na kitolea sumu mfano wa sindano kali kwenye mkia wake.

Na nguvu zote dhidi ya adui

Nimewapa mamlaka kuzishinda nguvu za adui" au " Nimewapa mamlaka ya kumshinda adui" na adui ni Shetani.

Msifurahi tu katika hili,kwamba roho wanawatii

" Msifurahi tu kwa sababu wanawatii"'

majina yenu yameandikwa mbinguni.

AT: "Mungu ameyaandika majina yenu mbinguni" au "Majina yenu yapo katika orodha ya watu ambao ni ufalme wa mbinguni".

Luke 10:21

Bwana wa mbingu na dunia

AT: "Mtawala juu ya kilammoja na kilakitu mbinguni na duniani"

Vitu hivi

Hii inarejea mafundisho ya nyuma ya Yesu juu ya mamlaka ya wanafunzi wake. Inaweza kuwa rahisi kusema " vitu hivi" na msomi aweze kuielewa maana.

Wenye hekima na ufahamu

" kutoka kwa watu wenye hekima na ufahamu". AT: "kutoka kwa watu wanaofikiri kuwa waoni wenye hekima na ufahamu".

kwa wasio fundishwa

Hii inamaanisha wale watu wasio waza kuwa wao ni wenye hekima na wanawiwa kuyapokea mafundisho ya Yesu.

Kama watoto wadogo

"kama watoto wadogo". hii inawakilisha watu wanaojua ya kuwa si wenye hekima na maarifa.

kwa kuwa ilikuwa nzuri na kupendeza katika macho yako.

SAT: "kwa nyie mkiyafanya haya, yanawapendeza ninyi".

Luke 10:22

Kila kitu kimekabithiwa kwangu kutoka kwa Baba yangu

AT: " Baba yangu amekabidhi kila kitu kwangu".

Baba... Mwana.

Hivi ni vichwa vikuu vya muhimu vinavyoelezea uhusiano kati ya Mungu na Yesu.

Mwana

Yesu alikuwa akijizungumzia yeye katika nafasi ya tatu.

afahamuye Mwana ni nani

Neno ambalo limetafasiriwa kama "Afahamuye" linamaanisha kujua kutokana na kumwelewa mtu. Mungu Baba anamjua Yesu kwa namna hiyo.

Ila Baba

Hii inamaanisha ni Baba peke yake anajua Mwana ni nani.

na yeyote ambaye mwana anatamani kujifunua kwake

AT: "na watu watajua Baba ni nani endapo Mwana atataka kuwadhihirishia Baba kwao".

Luke 10:23

Akawageukia wanafunzi, akasema kwa siri,

Yawezekana hii ilikuwa katika wakati fulani. AT: "badaye, ambapo wanafunzi wakewalikuwa peke yao pamoja naye, akasema"

Wamebarikiwa wavionavyo vitu mvionavyo

Pengine hii ilikuwa na maana kwa watu wote waliokuwa wamekuja kumsikiliza Yesu AT: "Ni jinsi gani ilivyo vyema kwa wale wanaoona vitu mnavyoviona".

Vitu hivi mvionavyo

"Vitu ambavyo mmeniona mimi nikivifanya"

Vitu hivi mvisikiavyo

"Vitu ambavyo mmenisikia mimi nikiviongea".

Luke 10:25

Sentensi unganishi

Yesu anajibu kwa kutumia simuilizi kwa mwalimu wa kiyahudi ambaye alitaka kumujaribu Yesu.

Tazama, mwalimu fulani

Hii pia ilitokea kwa wakati fulani, AT: "Siku moja Yesu alipokuwa akiwafundisha watu, Mwalimu fulani"(UDB)

Tazama

Hii inatupeleka moja kwa moja kwa mtu mpya katika simulizi. Pengine lugha yako ikawa ina namna ya kufanya hivi.

Alimujaribu

"Kumchanganya"

Kimeandikwa nini katika sheria?

Yesu anatumia mfano kumfundisha huyu Mwalimu wa kiyahudi. AT: "niambie ni nini Musa aliandika kwenye sheria"

Unaisoma je?

"Umesoma nini ndani yake?" au "Unaelewa nini ambacho unaweza sema?"

Lazima umpende.... jirani kama wewe mwenyewe

Mtu yule(myahudi) ananukuu kile Musa alichoandika kwenye sheria.

Moyo wako.....roho yako....nguvu zako...akili yako

Yote hii inamaanisha ya kuwa mtu lazima ampende Mungu kikamilifu na kila kitu chake

Jirani yako

Hii inamaanisha mtu aliepo katika jamii yako. AT: "raia mwenzako" au "watu wa jamii yako".

Luke 10:29

Lakini mwalimu, akitamani kujibibitisha kuwa

Lakini alijaribu kutafuta njia ya kujisafisha yeye mwenyewe, hivyo akasema" au " lakini akataka kuonekana kuwa ni mwenye haki, akasema"

Akajibu, Yesu akasema

Yesu akamjibu yule mtu kwa kumwambia fumbo AT: " kwa kumjibu Yesu akamwambia simulizi hii"

Akaangukia kati ya wanyang'anyi,

" Alizungukwa na wanyang'anyi" au "wanyang'anyi wakamteka".

Wakamvuaa na kumnyang'anya vya kwake

"Walimchukulia vyote alivyokuwa navyo" au "Wakamuibia vitu vyake vyote"

Luke 10:31

Kwa bahati

Hiki ni kitu ambacho hakuna alikuwa amepanga.

kuhani fulani

Maelezo haya yanatambulisha mtu mpya katika simuilizi, lakini haimutaji kwa jina lake.

Na alipomuona

"Na baada ya kuhani kumuona yule mtu aliekuwa amejeruhiwa".Kuhani ni mtu wa dini, hivyo watu walihisi ya kuwa angemsaidia yule mtu.Kwa sababu hakumsaidia aya hii ingeweza kutafasiriwa kama "lakini baaada ya kumuona" kuleta umakini kwa hii hali ambayo haikutokea kama ilivyokuwa ikitarajiwa.

Akapita uapende mwingine wa barabara

Inaonesha dhahiri ya kuwa hakumsaidia yule mtu mwenye majeraha. AT:"hakumsaidia yule mwenye majeraha badala yake alimpita".

Luke 10:33

Lakini msamaria mmoja

Hii inatambulisha mtu mpya kwenye simulizi bila ya kutaja jina lake. Tunajua tu ya kuwa alikuwa msamaria . Wayahudi walikuwa wakiwadharau wasamaria na walikuwa wakimudhania ya kuwa hatamsaidia yule myahudi aliekuwa ameumizwa.

Alipomuona

"Baada ya msamaria kumuona yule mtu aliekuwa ameumizwa"

Alisukumwa kwa huruma

"Akamuonea huruma"

Akamfunga vidonda vyake, akavimwagia mafuta na divai.

Angekuwa ameweka yale mafuta na divai kwenye vidonda vyake, AT:" akaweka divai na mafuta kwenye vidonda na akavisokota kwenye nguo"

Akavimwagia mafuta na divai

Divai ilitumika kusafisha vidonda na mafuta yalitumika kuzuia kudhuriwa kwa vidonda

Mnyaama wake

"Mnyama wake mwenyewe". Huyu alikuwa mnyamaambaye alitumika kubeba mizigo mizito. inasemekana alikuwa punda.

Dinari mbili

"Mshahara wa siku mbili". Denari ni umoja wa denari.

Mwenyeji wake.

" Mwangalizi wake" au "mtu ambaye alimtunza na kuwa akribu naye"

Luke 10:36

Ni yupi kati ya hawa watatu unafikiri.

AT:" Unafikiri nini? ni nani kati ya hawa watatu"

Alikuwa jirani

"Alijionesha mwenyewe kuwa jirani mwema"

Yeye alieangukia kati ya wanyang'anyi.

" Kakwe yeye ambaye wanyang'anyi walimteka"

Luke 10:38

Taarifa kamili

Yesu anakuja kwenye nyumba ya Matha ambapo dada yake Mariam akawa akimsikiliza Yesu kwa umakini mkubwa.

sasa

Neno hili limetumika mahali hapa kuonesha tukio jipya

walipokuwa wakisafiri,

"Kama ambavyo Yesu na wanafunzi wake walikuwa wakisafiri"

kijiji fulani

Hii inatambulisha kijiji kama sehemu mpya,lakini hapakupewa jina.

mwanamke mmoja jina lake Matha

Hii inamtambulisha Matha kama mhusika mpya. Pengine lugha yako ikawa na namna nyingine ya kumtambulisha mtu mpya.

alikaa miguuni mwa Bwana

Hii ilikuwa kawaida na yenye heshima kwa mtu anayetaka kujifunza kwa mda ule. AT:" alikaa kwenye sakafu"

na kusikiliza neno lake

AT: "Na akasikiliza Mafundisho ya Bwana"

Luke 10:40

haujali...peke yangu?

Martha alaikuwa analalamika kuwa Bwana alimruhusu Mariamu aketi amsikilize wakati kulikuwa na kazi nyingi za kufanya. Alimuheshimu Bwana, ndo maana alitumia swali la kejeli kufanya malaliko yake kuwa ya upole.AT: "inaonekana hujali..pekeyangu."

Martha, Martha

Yesu arudia rudia jian la martha kuonesha msisitizo. AT: "Mpendwa Martha" au "wewe Martha."

ambacho hakitachukuliwa kutoka kwake

Inaweza maanisha 1) " Sitachukua fursa yake" au "2) "Hatapoteza alichopatakwa sababu ananisikiliza."

Luke 11

Luka 11 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri hupendelea kuweka mbele kidogo mashairi au sala maalum. ULB na tafsiri nyingine nyingi za Kiingereza huingiza mistari ya 11: 2-4, ambayo ni sala maalum, inayoitwa "Sala ya Bwana." Sala hii katika Mathayo 6 kuweka mbele kidogo."

Dhana maalum katika sura hii

Sala ya Bwana

Huu sio maombi ya kurudiwa mara kwa mara, ingawa sala hii inaweza kutumika kwa njia hiyo. Badala yake, hutoa mfano wa jinsi Wakristo wanapaswa kuomba.

Yona

Yona alikuwa nabii wa Agano la Kale wa muhimu fulani lakini sio umuhimu mkubwa. Aliita taifa la Wayunani kutubu dhambi zao na walitii. Matukio haya husababisha nabii wa Kiyahudi kuwa na hasira juu ya neema ya Mungu inayoonyeshwa kwa Mataifa. Sura hii inalinganisha na mtazamo wa baadaye wa Wayahudi, sababu ya ukosefu wao wa toba na baadaye kuwa na hasira juu ya Mungu kwa neema anayowaonyesha Wayunani. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#prophet, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#grace)

Mwanga

Mwangazi ni picha ya kawaida katika Maandiko iliyotumiwa kuonyesha haki. Mwanga pia hutumiwa kuonyesha njia ya haki na kuonyesha kuishi kwa haki. Giza mara nyingi hutumiwa kama picha ya kuonyesha dhambi au uovu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#unrighteous)

Kuosha

Hii ilikuwa zoezi lililofanywa na Mafarisayo, lakini haikuwa wajibu kulingana na sheria ya Musa. Mafarisayo walikuwa na ibada nyingi zinazohusisha kuosha kwa kujaribu kujiweka safi. Hii ni ajabu kwa sababu hakuna kiasi cha maji kinachoweza kuwafanya kuwa safi kiroho. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lawofmoses, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#clean and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-irony)

<< | >>

Luke 11:1

Habari za jumla

Hii ni mwanzo wa sehemu inayofuata ya hadidhi. Yesu aliwafundisha wanafunzi wake kuomba

Ilitokea

Neno hili lilitumika kuonyesha mwanzo wa...

Luke 11:2

Yesu akawaambia, "msalipo mseme, "Baba Jina lako litakaswe

Yesu, mwana wa Mungu, Aliwaamuru wanfunzi kuheshimu Jina la Mungu "Baba", kwa kulitamka jina la Mungu kama "Baba" wakati wa kuomba

Yesu akawaambia

Yesu aliwaambia wanafunzi wake

Baba

Hii ni cheo muhimu kwa Mungu

Jina lako litakaswe

"Watu wote wakuheshimu wewe" au "mfanye kila mmoja aliheshimu Jina lako"

Ufalme wako uje

"Uizimamishe ufalme wako" Tunataka utawale watu wako.

Luke 11:3

Maneno yenye kuunganisha

Yesu aliendelea kuwafundisha wanafunzi wake namna ya kuomba.

mkate wetu wa kila siku

Mkate ni chakula cha gharama ambacho huliwa na watu kila siku

Utusamehe makosa yetu

"Utusamehe kwa kufanya dhambi kinyume na wewe" au "Tusamehe dhambi zetu"

Kama nasi tunavyo wasamehe

Kwasbabu nasi tunawasamehe

Waliotukosea

wale waliofanya makosa juu yetu au waliotutendea mambo mabaya

Usituongoze katika Majaribu

Tuongoze mbali na majaribu

Luke 11:5

Maneno yenye kuunganisha

Yesu aliendelea kufundisha wanafunzi wake juu ya maombi

Ni nani kati yenu mwenye

Yesu alitumia maswali kuwafundisha wanafunzi wake . "Fikiria mmoja wenu anayo" au "Fikiria unayo"

Niazime mikate mitatu

Nikopeshe mkate mitatu au nipe mikate mitatu na nitakupilia baadaye . Mwenyeji hana chakula chochote kilicho tayari cha kumpa mgeni wake.

amenijia sasa hivi kutoka njiani

alikuwa akisafiri na sasa hivi akaja nyumbani mwangu

sina cha kumuandalia yeye

"chakula chochote kilicho tayari cha kumpa"

Siwezi kuamuka

"Siyo rahisi kwangu mimi kuamka"

Nawaambia

Yesu alikuwa akiongea na wanafunzi, Neno ninyi ni wingi

akupe mkate kwasababu wewe ni rafiki yake

Yesu aliongea na wanafunzi wake kana kwamba wao ndiyo waliokwenda kuomba mkate.

kuendelea bila aibu

Hii inamaanisha ile hali ambayo yule mtu aliendelea kuomba mkate bila kujali kama ni wakati mwafaka wa rafiki wake kuamka katikati ya usiku na kumpa mkate

Luke 11:9

Omba..tafuta....bisha

Yesu alitoa hizi amri kuwatia moyo wanafunzi wake kuomba bila kukoma. Lugha nyingine huitaji maelezo zaidi. "waweza kuelezea kama ifuatavyo: endelea kuomba kwa kile unachokihitaji....endelea kutafuta kile unachohitaji kwa Mungu...endelea kubisha hodi kwenye mlango"

Nanyi mtapewa

"Mungu atakupatia " au "Utapokea"

Bisha/kugonga

Kugonga katika mlango ni kupiga mara kadhaa kumfanya yule aliyeko ndani ajue kuwa unasimama je. Inaweza pia kutafsiriwa kwa kutumia njia ambayo watu wa kabila lenu huonyesha kuwa wamefika. Mfano "Kuita" au "kukohoa" au "Kupiga makofi" . Hapa inamaana mtu anendelee kuomba kwa Mungu hadi amjibu

itafunguliwa kwenu

"Mungu atafungua Mlango kwa ajili yako" au "Mungu atakukaribisha Ndani"

Luke 11:11

kauli inayounganisha

Yesu alimaliza kufundisha wanafunzi wake kuhusu maombi.

Nani kati yenu...nyoka?

Yesu alitumia maswali kufundisha wanafunzi wake. " Hamna kati yenu...nyoka"

Mkate

"Mkate" au "Kiasi cha cakula"

au badalaya samaki, nyoka?

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. "Au, kama akiomba samaki, hutampa nyoka"

Nnge

Nge ni kama buibui , lakini ana mkia wenye sumu unao choma. Kama Nnge hafahamiki sehemu unayoishi, waweza kutafsiri kama "buibui mwenye sumu" au "Buibu anayechoma"

kama ninyi mlio waovu mnajua

"kwa kuwa ninyi mlio waovu mnajua " au "hata japokuwa ninyi ni watenda dhambi , mnajua"

Je si zaidi Baba yenu wa mbinguni atawapa na kuzidi Roho Mtakatifu ... wamuombao?

Je si zaidi na kwa uhakika Baba yenu wa mbinguni atawapa Roho Mtakatifu ...Yeye? Yesu alitumia maswali tena kuwafundisha wanafunzi wake. "Uwe na uhakika kuwa Baba yenu wa Mbinguni atawapatia Roho Mtakatifu...yeye"

Luke 11:14

Habari ya Jumla

Hii ni sehemu nyingine ya hadithi iliyofuata. Yesu alihojiwa baada ya kukemea pepo limtoke kwa mtu aliyekuwa bubu.

Yesu alikuwa akimuondoa pepo

"Yesu alikuwa akimuondoa pepo nje ya mtu" Au " Yesu alimuamuru pepo kumuacha mtu"

alikuwa bubu

hunda yule pepo haongei. Huenda msomaji alifahamu kuwa huyo pepo alikuwa na nguvu ya kuwafanya watu wasiongee. " pepo alimsababishia yule mtu asiweze kuongea"

ikawa

kifungu hiki inatumika kuonyesha tendo lilipoanza. Kama lugha yenu ina namna ya kufanya hili, unaweza kutumia hapa. Pepo alipomtoka mtu yule, na hivyo ikampelekea Yesu kufundisha habari za roho mbaya.

ikawa pepo lilipomtoka

"wakati pepo lilipo mtoka mtu" au "wakati pepo lilipo muacha mtu"

yule mtu aliyekuwa bubu akazungumza

"mtu ambaye alikuwa hawezi kuzungumza sasa akazungumza"

Kwa Beelzebul, mkuu wa mapepo, anatoa mapepo

"anatoa mapepo kwa nguvu ya Beelzebul, mkuu wa mapepo"

Luke 11:16

Habari ya jumla

Yesu alianza kujibu umati waliojikusanya

Wengine wakamjaribu

"Watu wngine walimjaribu Yesu". Walimtaka awathibitishie kuwa mamlaka yake yanatoka kwa Mungu.

na kumtaka awaonyeshe ishara kutoka mbinguni

"na kumuambia awape ishara kutoka mbinguni" au "kwa kutaka awaonyeshe ishara kutoka mbinguni". Ni kwa njia hii walimtaka yeye athibitishe kuwa mamlaka yake yanatoka kwa Mungu.

Kila ufalme utakaogawanyika itakuwa ukiwa

"Kama watu katika ufalime watapigana wenyewe kwa wenyewe, wataingamiza ufalme wao. "

Nyumba iliyogawanyika itaanguka

Hapa "Nyumba" inamaanisha ni familia, "Kama watu wa familia moja wakipigana wenyewe kwa wenyewe wataiharibu familia yao"

kuanguka

"Kuangushwa chini na kuharibiwa" Taswira hii ya nyumba kuanguka chini inafananishwa na uharibifu utakaotokea pale watu wa familia moja wakipigana wenyewe kwa wenyewe.

Luke 11:18

kama shetani takuwa amegawanyika

"Shetani" hapa inawakilisha wale mapepo waliojiunga na Shetani kumuasi Mungu. "Kama shetani na washirika wa ufalme wake wanapigan a wao kwa wao"

ufalme wake utasimamaje?

Yesu alitumia maswali kufundisha watu. "Ufalme wa Shetani hautadumu" au "Ufalme wa shetani utaanguka na kusambaratika"

Kwasababu mwasema natoa mapepo kwa Belzebuli

Kwa sababu mwasema ni kwa nguvu ya Belzebuli nawafanya mapepo kuwaacha watu . sehemu iliyofuata ya majibu yake inaweza kutamkwa kirahisi: "hii inamaana Shetani amegawachika juu yake"

Je wenzenu wanatoa mapepo kwa njia gani?

"ni kwa nguvu ya nani wenzenu wanawaamurisha mapepo kuwaacha watu. " Yesu alitumia swali kufundisha watu.Swali la Yesu inaweza kurahisishwa, "basi ni lazima tukubaliane kuwa wenzenu pia hutumia nguvu ya Beelzebuli kuondoa mapepo". "Lakini tunajua kuwa hiyo si kweli".

wao watawahukumu ninyi

wenzenu wanao watoa mapepo kwa nguvu ya Mungu watawahukumu ninyi kwa kusema kuwa mimi natoa mapepo kwa nguvu ya Beelzebuli.

kwa kidole cha Mungu

"Kidole cha Mungu" inamaanisha ni Nguvu ya Mungu

Basi ufalme wa Mungu umewajia

"Hii inaonyesha kuwa ufalme wa Mungu umekuja kwenu"

Luke 11:21

mtu mwenye nguvu ...akilinda nyumba yake

Hii inaongelea Yesu ambaye anamshinda Shetani na mapepo wake kama mtu mwenye nguvu zaidi ananyo chukua vitu vya mtu mwenye nguvu

vitu vyake vitakaa salama

"hakuna awezaye kuiba vitu vyake"

na kuzichukua mali zake zote

"Kuiba mali zake" au kuchukua kila kitu alichokitaka"

yeye asiye pamoja nami

"yeye asiyenisaidia " au "yeye asitenda kazi pamoja nami"

yuko kinyume nami

"anafanya kazi kinyume nami". Hii inamaanisha wale watu waliosema kuwa Yesu anafanya kazi pamoja na Shetani.

Luke 11:24

mahali pasipo maji

"Hii inamaanisha "sehemu ya ukiwa", mahali ambapo roho mbaya hurandaranda .

akikosa

"kama roho hakupata sehemu ya kupumzika"

nyumba yangu nilikotokea

Hii inamaanisha mtu yule ambaye alikuwa anakaa kwake. "mtu ambaye nilikuwa nikikaa kwake"

na kukuta nyumba imefagiliwa na imekaa vizuri

"akaikuta mtu alifagia nyumba na kuwa safi na kuweka kila kitu mahali pake " au " kumkuta mtu kama nyumba iliyosafishwa na kupangiliwa vizuri"

imefagiliwa

"tupu" Mfano huu inamaanisha hali ambayo mtu hakujazwa Roho wa Mungu baada ya mapepo kuondoka.

Luke 11:27

Habari ya Jumla

Huu ni mkatizo wa mafindisho wa Yesu. Mwanamke aliongea baraka na Yesu akajibu.

Ilitokea

Kifungu hiki kinatumika kuonyesha tukio muhimu katika historia. Kama lugha yako ina njia ya kufanya hii, unaweza ukatumia hapa.

aliyepasa sauti yake kwenye mkutano

"aliongea kwa sauti iliyozidi kelele za umati"

Limebarikiwa tumbo lililo kuzaa na matiti ulioyanyonya

Sehemu ya mwili wa mwanamke ilitumika kuwakilisha mwanamke. " Ana heri kiasi gani yule mama aliyekuzaa na kukunyonyesha kwenye matiti yake" au " Ana furaha iliyoje yule mwanamke aliyekuzaa na kukunyonyesha kwenye matiti yake"

lakini, wamebarikiwa wale

" Ni vizuri zaidi kwa wale "

Luke 11:29

Kauli inayounganisha

Yesu aliendelea kufundisha umati

Kizazi hiki ni kizazi cha uovu

Watu wanaoishi katika nyaka hii ni watu waovu

Hutafuta ishara

"Wanataka mimi niwape ishara " au "Wengi wenu mnataka mimi niwape ishara" . Habari ya aina ya ishara wanayotaka inaweza kufaywa rahisi kama ilivyo katika UDB

na hakuna ishara watakao pewa

"Mungu hatawapa ishara "

Ishara wa Yona

"kile kilichotokea kwa Yona" au "muujiza ambao Mungu alifanya kwa Yona"

Maana kama Yona alivyokuwa ishara...ndivyo

Hii inamaana kuwa Yesu atatumika kama ishara kutoka kwa Mungu kwa ajili ya Wayahudi wa wakati huo kama ilivyokuwa kwa Yona alivyotumika kama ishara kutoka kwa Mungu kwa watu wa Ninawi.

Mwana wa Adamu

Yesu alikuwa akijisemea mwenyewe

Luke 11:31

Malkia wa Kusini

Hii ilimaanisha malkia wa wa Sheba. Sheba ilikuwa ni ufalme wa kusini mwa Israeli

atasimama siku ya hukumu na watu wa kizazi hiki

"Atasima pia na kuwahukumu watu wa kizazi hiki"

kalitoka katika mwisho wa nchi

"alikuja tokae umbali mrefu" au " Alikuja kutoka sehemu ya mbali"

Yuko mkuu kuliko Sulemani

Yesu alikuwa akiongelea juu yake. "Mimi ni mkuu kuliko Sulemani lakini hamnisikilizi"

Luke 11:32

Watu wa Ninawi watasimama katika hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki na kuwahukumu

"Watu wa Ninawi watasimama na kuwahukumu watu wa nyakati na kuwalaani."

kwani walitubu

"watu wa Ninawi walitubu"

Yuko aliye mkuu kuliko Yona

Yesu alijiongelea mwenyewe. "Mimi ni mkuu kuliko Yona lakini hamkutubu"

Luke 11:33

Kauli unayounganisha

Yesu alimaliza kuwafundisha makutano

Kuweka sehemu ya chini yenye giza

"kuficha kwenye sehemu iliyofichika"

Ila Juu ya kitu

"ila wanaweka juu ya meza" au " Ila wanaweka juu ya kabati"

Jicho lako ni taa ya mwili

Hii imewasilishwa na mafumbo tofauti. Jicho hufananishwa na Maono, ambayo ni mfano wa kuelewa. Mwili ni kiwakilishi cha maisha ya Mwanadamu. " Jicho lako ni taa ya maisha yako" au "Maono yako ni taa ya maisha yako" Kwasababu Yesu alikuwa anaongea kitu ambacho ni kweli kwa kila mtu, inaweza ikatafsiriwa kama " Jicho ni taa ya mwili wa mwanadamu"

Jicho lako likiwa zuri

" Maono yako yakiwa mazuri" au "ukiona vema"

mwili wako wote utakuwa kwenye mwanga

Yesu aliongelea kweli kama mwanga . "mwanga wa kweli utakuwa maishani mwako" Au "Maisha yako yote utakuwa na mwanga"

jicho lako likiwa baya , mwili wako wote utakuwa kwenye giza.

Yesu aliongelea habari ya kuwa katika uongo kama vile ni kuwa katika giza. " Maono yako yakiwa mabaya, basi maisha yako yote yanajawa na giza"

mwili wako wote utakuwa sawa na mwanga utouo mwango kwenu.

Yesu aliongea watu ambao wamejawa na kweli kama vile taa iwakavyo na kutoa mwanga wote.

Luke 11:37

Habari ya Jumla

Huu ni mwanzo wa sehemu iliyofuata ya hadithi. Yesu alikaribishwa kula nyumbani mwa Mfarisayo

akawa pamoja nao

"kukaa katika meza". " ilikuwa ni desturi kwa chakula kama hii wanaume kula wakiwa wamekaa vizuri kwa kustarehe kwenye meza"

kunawa

Mafarisayo wana sheria ya kuwa watu ni lazima wanawe mikono yao ili waonekane kuwa wasafi mbele za Mungu. "kunawa mikono" au "kunawa mikono ili kuwa msafi kiibada"

Luke 11:39

Habari ya jumla

Yesu alianza kuongea na mafarisayo

nje ya vikombe na bakuli

Kuoasha nje ya vyombo ilikuwa ni sehemu ya mazoea ya ibada kwa Wafarisayo

lakini ndani yenu mmejaa tamaa na uovu.

Hii inafananishwa na njinzi wanavyosahau ndani ya vyombo na wanavyosahau maisha yao ya ndani.

Je yeye aliyeumba nje hakuumba na ndani pia?

Yesu alitumia swali kuwakemea Mafarisayo kwa kutojua ya kuwa kile kilichoko ndani ya miyoyo yao inajalisha kwa Mungu.

Wapeni maskini yaliyo ndani

"Wapeni Maskini kile kilichoko ndani ya vikombe na bakuli" au " Muwe wakarimu kwa watu maskini"

Luke 11:42

mnatoza zaka ya mnanaa na kila aina ya mboga ya bustani

" mnatoa moja ya kumi ya mnanaa na mchicha na kila aina ya mboga ya bustani", Yesu alikuwa anatoa mfano wa njinzi mafarisaya walivyo makini katika kutoa moja ya kumi ya mapato yao.

mnanaa na mchicha

hizi ni kama dawa. Watu huweka kidogo kwenye chakula ili kuipa utamu fulani. Kama watu hawafahamu mnanaa na mchicha, unaweza kutumia majina ya viungo wanayoijua au ufahamu wa jumla wa "viungo."

na kila aina ya viungo vya bustani

Tafsiri yake inaweza kuwa 1) Kila aina nyingine ya mbogamboga" 2) "Kila aina ya viungo vya bustani" 3) Kila aina ya mimea ya bustani

bila kuyaacha kuyafanya na hayo mengine pia

"na kila wakati myafanye na hayo mengine pia"

Luke 11:43

kauli inayounganisha

Yesu alimaliza kuongea na mafarisayo

viti vya mbele

"viti vizuri sana"

ole wenu, kwani mnafanana na makaburi yasiyo na alama ambayo watu hutembea juu yake pasipokujua"

Mafarisayo ni kama makaburi yasiyo na alama kwasababu wanaonekana kama waasafi, lakini huwafanya watu waliokaribu nao kuwa siyo wasafi.

makaburi yaliyofichika

Makaburi hayo yalikuwa mashimo kuchimbwa katika ardhi ambapo maiti kuzikwa. Wao hawakuwa na mawe nyeupe kwamba watu kawaida kuweka juu ya makaburi ili kwamba watu wengine kuona kwao. Wakati watu kutembea juu ya kaburi, wangeweza kuwa najisi.

Luke 11:45

Habari ya Jumla

Yesu alianza kumjibu mwalimu wa Kiyahudi

kwani mnawapa watu mizigomikubwa wasiyoweza kuibeba

"munaweka mizigo juu ya watu ambayo ni mizito kubebeka" . Yesu aliongea kuhusu mtu fulani kuwapa watu sheria nyingi kama mtu kuwapa mizigo mizito kubeba. "Mnawapa watu mizigo mizito kwa kuwapa sheria nyingi za kufuata"

walakini ninyi hamgusi mizigo hiyo hata kwa moja ya vidole vyenu.

"lakini hamtumii hata moja ya kidole chenu kuwasaidia kubeba mizigo hiyo. "Lakini hamfanyi kitu chochote kabisa kuwasaidia waitii sheria zenu"

Luke 11:47

ambao

Hii huwafanya kuona utofauti kati yao kwa namna wanavyo waheshimu manabii wakati wakipuuza ukweli kuwa wababu zao ndio waliowauwa.

hivyo ninyi mwashuhudia na kukubaliana

Yesu aliwakemea Mafarisayo na waalimu wa sheria . Walijua mauwaji ya manabii, lakini hawakushutumu wala kuwalaani wababu zao kwa kuwauwa. " kwahiyo, badala ya kuwakana wao, ninyi mwashuhudia na kukubaliana "

Luke 11:49

Kwasababu hiyo

Hii inarejea sentensi iliyofuata, Mungu atawatuma manabii wengi ili kuonesha kuwa kizazi hiki kitawauwa, kama walivyofanya baba zao.

Hekima ya Mungu inasema

"Mungu kwa hekima yake alisema" au "Mungu alisema kwa hekima"

Nitawatumia manabii na mitume

"Nitawatumia manabii na mitume watu wangu"

watawatesa na kuwauwa baadhi yao

"watu wangu watawatesa na kuwauwa baadhi ya manabii na mitume"

Kizazi hiki, kitawajibika na damu iliyomwagwa ya manabi wote.

Damu iliyomwagwa inamaanisha mauwaji ya manabii. "Kwa hiyo Mungu atawajibisha kizazi hiki kwa kifo cha manabii wote ambao watu wamewauwa"

Zakaria

Huyu ni kuhani wakati wa Agano la kale aliyewakemea watu wa israeli kwa habari ya usinzi. Huyu siye Baba wa Yohana Mbatizaji.

ambaye ameuwawa

"ambaye watu walimuuwa"

Luke 11:52

Kauli ya kuunganisha

Yesu alimaliza kumjibu mwalimu wa Kiyahudi

mmechukuwa funguo za ufahamu ...na mnawazuia wale wanaotaka kuingia

Yesu aliongea kuhusu ukweli wa Mungu kama vile ilikuwa ndani ya nyumba ambayo waalimu walikataa kuingia na hawaruhusu wengine kuingia. Hii ina maanisha waalimu hawamjui Mungu , na pia wanawazuia wengine kumjua Yeye pia.

Ufunguo

Hii inawakilisha maana ya ruhusa, kama kwenye nyumba au kwenye chumba cha stoo.

nyie wenyewe hamuingii

" ninyi wenyewe hamuingii ndani kupata ufahamu"

Luke 11:53

Habari za jumla

Huu ni mwisho wa sehemu ya hadithi ambapo Yesu alikula katika nyumba ya mfarisayo. Hii mistari inamweleza msomaji nini kilifanyika baada ya sehemu ya habari kuu ya hadithi kuisha "

Baada ya Yesu kuondoka pale

" Baada ya Yesu kuondoka katika nyumba ya mfarisayo"

wakijaribu kumtega kwa maneno yake

Hii inamaanisha walihitaji Yesu kusema kitu kibaya ili waweze kumshitaki

Luke 12

Luka 12 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

"Kukufuru Roho"

Kuna matatizo mengi juu ya kutambua vizuri dhambi hii maalum. Hata hivyo, inaonekana kuwa inahusisha kumtukana Roho Mtakatifu na kazi yake. Kwa kuwa sehemu ya kazi yake ni kuwashawishi watu juu ya dhambi zao na kwamba wanahitaji kusamehewa na Mungu, yeyote anayezarau ukweli huu, atakataa kuja kwa Mungu kwa toba. Kwa sababu hii, hangeweza kusamehewa. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

Usimamizi

Ingawa neno "msimamizi" haitumiwi katika sura hii, uwakilishi, ambao ni kazi ya msimamizi, ni neno kubwa katika mafundisho haya. Msimamizi mwema ni mtu ambaye wengine wanaweza kumwamini kushughulika juu ya vitu vyao. Kwa sababu kila kitu ni cha Mungu daima, kila kitu anachompa kila mtu bado ni cha Mungu, na mtu anayepokea zawadi kutoka kwa Mungu ni mwendeshaji wa kile ambacho ni cha Mungu. zawadi kwa Mungu" instead of "zawadi kutoka kwa kwa Mungu" or "Hivi sivyo vitu vinavyoonekana tu, vitu ambavyo Mungu aliwaruhusu mtu kuchunga, lakini ni mambo pia kama uwezo wa asili wa mtu huyo. Mungu anatumaini kama watumishi wake watakumbuka kama ataweza kila mara kuwaomba ripoti ya vitu alivyowapatia. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#trust)

Mgawanyiko

Kuna fundisho muhimu juu ya mgawanyiko katika sura hii (Luka 12:51-56). Mgawanyiko huu haukusudi kuwa na maana ya kusema kama watu wangekuwa adui. Lakini, ina maana ya kusema kama katika ulimwengu kuna mgawanyiko wazi kati ya watu Wakristo na watu wasio Wakristo na wale wasio Wakristo. Kuonekan kama mfuasi wa Yesu ni muhimu kuliko uhusiano nyingine wowote wa familia.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Mwana wa Binadamu"

Yesu anajiita mwenyewe kama "Mwana wa Binadamu." Lugha zingine haziwezi kuruhusu mtu kujitaja mwenyewe kama 'mtu wa tatu.' (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sonofman)

Maelekezo ya jumla na Maalum

Mara na mara Agano Jipya hutoa maagizo au amri maalum kuhusu Wakristo wote. Wakati mwingine, maagizo yake yanafikiriwa kuwa maagizo ya ujumla na yanapaswa kuchukuliwa kama "mawazo mazuri." Kwa mfano, "usiwe na wasiwasi" au "uza vitu vyako" sio maagizo kwa Wakristo wote.

<< | >>

Luke 12:1

Habari za Jumla

Hii ni sehemu iliyofuata ya hadithi. Yesu alianza kuwafundisha wanafunzi wake mbele ya maelfu ya watu.

kwa wakati huo

"wakati wakifanya hayo "

wakati maelfu ya watu ..walikanyagana

Hii ni habari ya nyuma inayoelezea mpangilio wa hadithi

watu wengi maelfu

"ni kusanyiko kubwa"

walikanyagana

Hii ni kivumishi kinachoelezea wingi wa watu waliokuwepo

Alianza kusema na wanafunzi wake kwanza

"Yesu alianza kwanza kuongea na wannafunzi wake, na kuwaambia"

Mjihadhari na chachu ya Mafarisayo ambayo ni unafiki.

Kama vile chachu inavyoenea kwa donge la unga wa mkate, unafiki wao huenea kwa jamii nzima. "Mjitunze na unafiki ya Mafarisayo ambayo ni sawa na chachu" au " Mjihadhari msije mkawa wanafiki kama Mapharisayo. Hii tabia ya uovu hushawishi kila mmoja kama ambavyo chachu huharibu donge la unga"

Luke 12:2

Lakini hapatakuwepo na siri iliyofichika ambayo haitafunuliwa

"Lakini kila kitu kilichofichwa kitaonyeshwa" Neno "lakini" ni neno la kiunganishi" Lakini watu watajua mambo yote wafanyayo watu kwa siri"

wala jambo lililo fichwa ambalo halitajulikana

Hii ina maana sawa na sehemu ya kwanza ya sentensi ili kuzizitiza ukweli. " na watu watajifunza kuhusu kile ambacho watu wengine wanajaribu kuficha"

itasikiwa katika mwanga

" watu watasikia katika mwanga"

mliyoyasema kwenye sikio

"Kumnong'onezea mtu mwingine"

ndani ya vyumba vyenu vya ndani

"kwenye chumba iliyofungwa". "Kwa sehemu ya faragha" au "Kwa siri"

vitatangazwa

"itasemwa kwa sauti ya juu". "Watu watatangaza"

juu ya nyumba

Nyumba katika Israeli zlikuwa na paa gorofa, hivyo watu wanaweza kwenda na kusimama juu yao. Kama viongozi wanavyokuwa na wasiwasi kujaribu kufikiria jinsi watu wanavyoweza kupanda juu ya zile nyumba, hii inaweza pia kutafsiriwa na usemi zaidi kwaa jumla, kama vile "kutoka mahali pa juu ambapo kila mmoja atakuwa na uwezo wa kusikia."

Luke 12:4

Nawaambia rafiki zangu

Yesu anawaanda wasikilizaji wake kutambua kuhamia kwenye mada nyingine, kwa hili, kuongelea kuhusu kutokuogopa.

hawana kitu kingine cha kufanya

"hawawezi kusababisha maumivu mengine zaidi" au "hawawezi kukuzuru zaidi"

Muogopeni yule

"Mwogopeni Mungu ambaye" au "Muogopeni Mungu kwa sababu"

akisha kuua

"baada ya kukua" au "baada ya kumuua mtu"

ana mamlaka ya kutupa kwenye jehanamu

"ana mamlaka ya kuwatupa watu kwenye jehanamu"

Luke 12:6

Je shomoro watano hawauzwi kwa senti mbili?

Yesu anatumia swali kuwafundisha wanafunzi

Shomoro

Ni ndege wadogo sana wenye kula mbegu

hakuna mmoja wao atakayesahaulika mbele za Mungu

"Mungu hajawahi kusahau mmoja wao". "Mungu kwa uhakika anakumbuka kila shomoro"

hata nywele za vichwa vyenu vimehesabiwa

"Mungu anajua hata idadi ya nywele zilizoko kichwani mwako"

Msiogope

"Msiwaogope watu" au "Msiwaogope watu watakao waujeruhi ninyi"

Ninyi ni wa thamani kubwa kuliko shomoro wengi.

"Mungu anawathamini ninyi kuliko mashomoro wengi"

Luke 12:8

Nawaambia Ninyi

Yesu alikuwa anawaanda wasikilizaji wake kutambua kuhamia kwa mada nyingine, kwa hili, anaongelea kuhusu kukiri.

yeyote atakayenikiri mbele za watu

"yeye atakaye waambia wengine kuwa yeye nimwanafunzi wangu" au " yeyote atakaye nitambulisha mbele ya wengine kwamba ni mwaminifu kwangu"

Mwana wa Adamu

Yesu alikuwa akirejea Yeye mwenyewe. Mimi Mwana wa Adamu

yeyote atakaye nikana mbele za watu

"Yeyote atakaye nikataa mbele za watu" " Yeyote atakaye kataa kunitambulisha kwa wengine kuwa yeye ni mwanafunzi wangu" au " yeyote atakaye kataa kusema yeye ni mwaminifu kwangu"

naye atakanwa

"Atakanwa" Mwana wa Adamu atamkana yeye " au " Nitamkana kuwa si mwanafunzi wangu"

Yeyote atakayesema neno baya juu ya Mwana wa Adamu,

"Yeyote atakayesema jambo baya juu ya Mwana wa Adamu "

atasamehewa

"atasamehewa". "Mungu atamsamehe yeye kwa hilo"

atakayemkufuru Roho Mtakatifu

"atakayeongea maovu juu ya Roho Mtakatifu " au "Kusema kuwa Roho Mtakatifu ni mwovu"

Hatasamehewa

"Mungu atamuhesabu kuwa na hatia milele"

Luke 12:11

mbele ya wakuu wa masinagogi

" Ndani ya masinagogi ili wawaulize maswali kwa viongozi wa kidini"

wenye mamlaka

"watu wengine wenye nguvu ndani ya nchi"

kwa wakati huo

"kwa muda huo" au "Kisha"

Luke 12:13

Habari za Jumla

Hii ni katizo kwa mafundisho ya Yesu. Mtu mmoja alimuomba Yesu amfanyie kitu na Yesu akamjibu.

Mtu

Maana inayowezekani ni 1) Hii ni namna ya kuongea na mtu mgeni au 2) Yesu anamkemea yule mtu. Labda lugha yenu ina njia mbadala ya kuongea na watu kwa namna ya njia hizi mbili. Watu wengine hawatafsiri neno hili kabisa.

Ni nani aliyeniweka kuwa mwamuzi au mpatanishi kati yenu?

Yesu alitumia swali kumfundisha huyo mtu. " Mimi siyo mwamuzi wenu au mpatanishi" . Lugha zingine hutumia wingi wa maneno ya "Yenu" au "Wenu"

Ndipo akawaambia

Neno "akawaambia" hapa huenda inarejea umati wote wa watu.

jihadharini na kila namna ya tamaa

"Jichungei na kila aina ya uchoyo". "Msijiruhusu kupenda kuwa vitu"au " Msiruhusu tamaa ya kuwa na vitu vingi iwatawale"

uzima wa mtu

Hii ni kauli ya jumla za ukweli. Haimrejei mtu yeyote maalum. Lugha nyingine zina jinsi ya kuelezea .

wingi wa vitu alivyo navyo

"Ni kiasi gani vya vitu anavyomiliki" au "kiasi gani ya mali anayomiliki"

Luke 12:16

Kauli inayounganisha

Yesu aliendeleza mafundisho yake kwa kuwaeleza mfano

Kisha Yesu akawaambia

Huenda Yesu alikuwa bado anaongea na mkutano wote.

ilizaa sana

"imezaa mavuno mengi"

ghala

jengo ambalo wakulima huhifadhi mazao na chakula wanachopanda baada ya kuvunwa

vitu

"Mali"

Nitaiambia nafsi yangu

"Nitajiambia mwenyewe"

Luke 12:20

kauli inayounganisha

Yesu alinukuu jinsi Mungu alivyomjibu mtu tajiri, alipokuwa anamalizia hadithi yake.

usiku wa leo wanahitaji roho kutoka kwako

"utakufa usiku wa leo" au " Nitaichukuwa uhai wako kutoka kwako leo"

na vitu vyote ulivyoviandaa vitakuwa vya nani?

"nani atamiliki vitu ulivyo hifadhi?" au " ni nani atakayekuwa nayo vitu ulivyoviandaa?" Mungu alitumia swali kumfanya mtu atambue kuwa hatamiliki tena vitu hivyo.

anayejiwekea mali

"kuhifadhi vitu vya dhamani"

na si tajiri

"maskini"

kwa ajili ya Mungu

Maana yake ni kwamba mtu huyu hakuwa anajali vitu vilivyo muhimu kwa Mungu, au kuwa Mungu atamlipa. "kwa mtazamo wa Mungu" au "kulingana na Mungu"

Luke 12:22

Kauli inayounganisha

Yesu aliendelea kuwafundisha wanafunzi wake mbele ya umati.

Kwahiyo

"kwasababu hiyo" au " kwasababu ya mafundisho ya hadihi hii"

Nawaambia

"Nataka niwaambie kitu muhimu"au "Inabidi msikilize kwa umakini juu ya hili"

juu ya maisha yenu-ya kuwa mtakula nini

"kuhusu maisha yenu na nini mtakula" au " kuhusu kuwa na chakula cha kutosha ili muweze kuishi"

juu ya miili yenu -ya kuwa mtavaa nini

"kuhusu miili yenu na nini mtavaa" au " kuhusu kuwa na nguo za kutosha za kuvisha miili yenu"

Luke 12:24

ndege wa angani (Rivens)

(Rivens) hii inamaanisha 1) Ni aina ya ndege wanaokula mbegu zaidi, au 2) aina ya ndenge wanaokula nyama ya wanyama waliokufa. Wasikilizaji wa Yesu watakuwa wameidharau hao ndege kuwa si kutu (rivens) kwani Wayahudi hawali aina hiyo ya ndege.

Ninyi si bora zadi kuliko hao ndege

Hii ni tahamaki na siyo swali. Yesu alisisitiza ukweli kwamba watu ni wa muhimu sana kwa Mungu kuliko ndege.

Ni yupi kati yenu ...maisha yake?

Yesu alitumia swali kufundisha wanafunzi wake

kuongeza dhiraa moja katika maisha yake

Huu ni mfano kwasababu dhiraa hutumika kupima urefu, na siyo muda. Taswira ya maisha ya mtu kufutwa kama vile ubao, au kamba , au kitu chochote kigumu.

ikiwa basi hamuwezi kufanya....hayo mengine ?

Yesu alitumia swali lingine kuwafundisha wanafunzi wake.

Luke 12:27

maua

(Lilies), haya ni mauwa mazuri yanayojiotea yenyewe shambani. Kama lugha yako haina jina la mauwa ya aina ya (lily) unaweza kutumia jina lingie la maua yanayofanana na hilo au tafsiri kama "maua"

wala hayajisokoti

"haitengenezi uzi ili yajivike" au "hawatengenezi uzi"

Sulemani katika utukufu wake

"Sulemani aliyekuwa na mali nyingi" au "Sulemani aliyevikwa vizuri"

Kama Mungu huyavika vizuri majani ya kondeni

"Kama Mungu huyavika majani ya kondeni namna hiyo " au "Kama Mungu huwapa mauwa ya kondeni mavazi mazuri hivyo" Kama Mungu hufanya majani ya kondoni kuwa mazuri kama hivi"

hutupwa kwenye moto

"mtu huzitupa kwenye moto"

Je si zaidi atawavika ninyi

"Hii ni mshangao na siyo swali. Yesu alitilia mkazo kuwa atawatunza na kuwajali watu zaidi kuliko anavyojali majani.

Luke 12:29

Msisumbukie juu ya kuwa mtakula nini au mtakunywa nini

"usitazame zaidi juu ya kula na kunywa" au "Msiwe na tamaa zaidi ya kula na kunywa"

mataifa yote ya dunia

Hapa "mataifa" inamaanisha "wasio amnini" "Watu wote wa mataifa mengine" au "watu wote wasio amini duniani"

Baba yenu anajua ya kuwa mnahitaji vitu hivyo

Baba wa Yesu, Mungu Baba, pia hufanyika Baba wa wote watakao muamini Yesu.

Baba

Hii ni sifa muhimu sana kwa Mungu.

Luke 12:31

tafuteni ufalme

"kushughulika na ufalme wa Mungu" au "Kutamani sana ufalme wa Mungu"

na hayo mengine mtazidishiwa

"hayo mambo mengine pia mtapewa". "Hayo mengine" ina maanisha chakula na mavazi. "Mungu atawapa ninyi hizo vitu"

kundi dogo

Yesu aliwaita wanafunzi wake kundi. Kundi ni mkusanyiko wa kondoo au mbuzi ambayo mchungaji anawatunza. Kama vile mchungaji anvyowajali kondoo, Mungu atawajali wanafunzi wa Yesu. "kundi dogo"au "kundi linalopendwa"

Luke 12:33

na mkawape maskini

"na wapeni watu maskini fedha mlizopata kwa mauzo"

mjifanyie mifuko ...hazina ya mbinguni

mifuko na hazina mbinguni zinamaanisha kitu kimoja. Vyote vinawakilisha baraka za Mungu mbinguni.

mjifanyie

"kwa namna hii mtajifanyia wenyewe"

mifuko isiyoishiwa

"mifuko ya fedha ambazo hazitoboki"

isiyokoma

'"ambazo haiishiwi" au "haipungui"

Moyo wako

Hapa "moyo" una maanisha mawazo ya mtu.

Luke 12:35

Kauli ya jumla

Yesu alianza kuelezea mfano

nguo zenu refu zifungwe na mkanda

Watu walivaa mavazi marefu. Walikuwa wakifunga na mkanda ili kuwafanya waweze kutembea njiani . " Funga nguo zako na mkanda ili uweze kuhudumia" au Uvae na uwe tayari kuhudumia"

taa zenu zihakikishwe kuwa zinaendelea kuwaka

"Fanyeni taa zenu ziendelee kuwaka"

muwe kama watu wanaomtazamia Bwana wao

Hii unafananishwa na jinsi wanafunzi wanavyotakiwa kuwa tayari kwa Yesu kurudi kama watumishi walio tayari kwa bwana wao kurudi.

kutoka kwenye karamu ya harusi

"kurudi nyumbani kutoka kwenye karamu ya harusi"

Luke 12:37

Wamebarikiwa

"Ni vizuri kama nini"

ambao bwana atawakuta wako macho akirudi

"wale ambao bwana wao atawakuta wakimngoja atakapo rudi" au "Walio tayari bwana akirudi"

atafunga ..atawaketisha chini

Kwasabu watumishi wamekuwa waaminifu na wako tayari kumuhudumia bwana wao, bwana atawalipa kwa kuwahudumia wao.

atafunga nguo yake refu na mkanda

'atajiandaa kuwahudumia wao kwa kufunga nguo yake na mkanda" au " atavaa tayari kuwahudumia"

kwa zamu ya pili ya ulinzi ya usiku

zamu ya pili ya ulinzi ni kati ya saa 3:00 usiku na saa 6:00 usiku. "karibu na usiku wa manane" au "kabla ya usiku wa manane"

au kwa zamu ta tatu ya ulinzi

zamu ya tatu ya ulinzi ni kuanzia saa 6:00 usiku na na saa 9:00 usiku. Au "akija akiwa amechelewa sana usiku"

Luke 12:39

asingeruhusu nyumba yake ifunjwe

"asingeruhusu mwizi aivunje nyumba yake"

kwani hamjui ni saa ngapi mwana wa Adamu atarudi

Kitu pekee kinacho wafananishwa kati ya mwizi na Mwana wa Adamu ni kwamba watu hawajui ni wakati gani wanakuja, hivyo wanatakiwa kuwa tayari.

wakati gani Mwana wa Adamu atarudi

Yesu alikuwa akiongelea habari zake mwenyewe. "wakati Mimi, Mwana wa Adamu, nitakapo kuja"

Luke 12:41

Kauli inayounganisha

Katika mstari wa 42, Yesu aliendelea kuelezea mfano

Kauli ya jumla

Katika mstari wa 41, kuna katizo katika kuelezea mfano kwani Petro alimuuliza Yesu swali kuhusu mfano.

Ni nani...kwa wakati mwafaka

Yesu alitumia swali kufundisha watu. Yesu hakujibu swali la Petro moja kwa moja, lakini alitegemea wale wanaotaka kuwa watumwa waaminifu kuwa mfano huo inawahusu wao. " Nimesema kwa kila mmoja ambaye ..kwa wakati mwafaka.

Mtumwa mwaminifu na mwenye hekima

Yesu alielezea mfano mwingine wa jinsi watumishi wanavyotakiwa kuwa waaminifu wakati wanamngoja bwana wao arudi.

ambaye bwana wake atamuweka juu ya watumishi wengine

"ambaye bwana wake atamuweka kuwa mtawala wa wengine"

Amebarikiwa mtumishi yule

"Itakuwa heri kwa mtumishi yule"

ambaye bwana wake akija atamkuta akifanya

"kama bwana wake akirudi atamkuta akifanya kazi hiyo"

Luke 12:45

Mtumishi yule

Hii ina maanisha yule mtumishi ambaye bwana alimuweka juu ya wengine

akisema moyoni mwake

"akafikiri ndani yake"

bwana wangu anakawia kurudi

"bwana wangu hatarudi mapema"

watumishi wa kiume na wa kike

Neno lililotafsiriwa hapa kama "watumishi wa kiume na Kike" mara nyingi hutafsiriwa kama "wavulana" na "wasichana". Inaweza kuashiri kuwa watumishi walikuwa vijana au wanao pendwa sana na bwana wao.

katika siku asiyotegemea

"wakati mtumishi hamtegemei"

kumuweka katika sehemu pamoja na wasio waaminifu

Inaweza kuwa na maana zifuatazo: 1) Ile hali ya bwana kutoa adhabu kali kwa mtumishi wake. 2) Hii inaelezea jinsi ambavyo mtumishi atakavyo vyongwa kama adhabu.

Luke 12:47

Kauli inayounganisha

Yesu alimaliza kuelezea mfano

atapigwa viboko vingi

"atapigwa mara nyingi" au "atachapwa mara nyingi" ."bwana wake atampiga mara nyingi"au "bwana wake atamuadhibu sana"

kwa kuwa yeye aliyepewa vingi, vingi hudaiwa kutoka kwake

"watahitaji vingi kwa yeyote aliyepokea vingi" au " bwana atahitaji vingi kwa kila mmoja aliyempa vingi"

na yeye aliyeaminiwa kwa vingi

"Kwa yule waliyempatia vitu vingi avitunze" au "kwa yule aliyepewa wajibu mkubwa"

aliyeaminiwa ...vitadaiwa

"bwana alimkabidhi ..bwana atataka"

Luke 12:49

Kauli inayounganisha

Yesu aliendelea kufundisha wanafunzi wake

Nimekuja kuwasha moto duniani

"Nimekuja kutupa moto duniani" au "Nimekuja kuwasha moto duniani" . Inawsza kuwa na maama zifuatazo: 1) Yesu alikuja kuwahukumu watu 2) Yesu alikuja kuwatakasa wanaomuamini 3) Yesu alikuja kusababisha kugawanyika kwa watu.

natamani iwe imekwisha kuwaka

Kuna msisitizo wa njisi alivyotaka hayo yatokee. " Natamani sana kuwa imeshawaka" au "Ni jinsi gani ninavyotamani iwe imeshaanza"

Lakini nina ubatizo ambao nitabatizwa kwayo

"Ubatizo" ina maanisha aina ya mateso ambayo Yesu atapata. Kama maji yamfinikavyo mtu wakati wa ubatizo, mateso yatamkabili na kumpata Yesu. " Ni lazima nipitie mateso mabaya" au "Nitapitia katika mateso makubwa kama vile mtu anavyofunikwa na maji wakati wa ubatizo"

Lakini

Neno "Lakini" linatumika kuonyesha kuwa hatawasha moto duniani mpaka kwanza apitie hayo mateso"

nina huzuni hadi ikamilike

Mshangao inasisitiza jinsi alivyo na huzuni. "Nina huzuni sana na itaendelea kuwepo hadi nimalize ubatizo huu wa mateso"

Luke 12:51

Je mnafikiri kuwa nimekuja kuleta amani duniani?

Yesu alitumia swali kufundisha wanafunzi wake. Watu walimtegemea Masiha awaletee amani kwa maadui wao. "Msifikiri kuwa nimekuja kuleta amani duniani"

lakini badala yake mgawanyiko

" lakini nimekuja kuleta mgawanyiko" au "watu watakuwa wakigawanyika miongoni mwao kwa sababu nimekuja"

mgawaniko

"uadui" au "kutoelewana"

kutakuwa na watu watano katika nyumba moja wamegawanyika

Hii ni mfano wa aina ya mgawanyiko utakao kuwepo kwenye familia.

kutakuwa na watano katika nyumba moja

kutakuwepo na watu watano katika nyumba moja

Luke 12:54

Kauli ya Jumla

Yesu alianza kuonge na umati

Nyakati za mvua zimewadia

"Mvua inakuja" au "Inaenda kunyesha"

nchi na anga

"nchi na anga" au " hali ya hewa"

inakuwaje hamuwezi kutafsiri nyakati za leo?

Yesu alitumia swali kukemea umati. "Mnatakiwa kujua namna ya kutafsiri nyakati za leo"

Luke 12:57

kwanini msihukumu yaliyo sahihi wenyewe?

Yesu anatumia swali kukemea umati. Anafundisha namna ya kufanya jambo jema kabila ya kuchelewa. Ninyi wenyewe mwatakiwa kutambua yaliyo mema"

wenyewe

"kwa utashi wenu" au "wakati bado mna muda wa kufanya hivyo"

Maana mkienda

Japo Yesu alikuwa akiongea na umati, hali aliyokuwa anaiwasilisha ni ya mtu kupitia mwenyewe..

kukubaliana na mshitaki wako

"mkubaliane juu ya jambo na mshitaki wako"

hakimu

Hili lina maanisha hakimu mkazi, lakini neno hili hap ni maalum zaidi na linatisha.

hatakutoa huko

"hatakuruhusu wewe utoke huko"

Luke 13

Luka 13 Maelezo ya Jumla

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Maarifa ya Kudhaniwa

Sura hii inaanza na kurejelea ya matukio mawili, ambayo maelezo yake hayajahifadhiwa (Luka 13:1-5). Ingawa hatujui habari yote ya matukio haya, wasomaji wa siku hizi wanafahamu vizuri mafundisho haya. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit) (Luka 13:1-5).

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Matumizi ya kitendawili

Kitendawili ni taarifa inayoonekana kuwa ya ajabu, ambayo ni kana kwamba inajikana yenyewe, lakini kwa hakika sio ya ajabu. Mfano wa kitendawili katika sura hii: "wale ambao hawana muhimu zaidi watakuwa wa kwanza, na wale ambao ni muhimu zaidi watakuwa wa mwisho" (Luka 13:30).

<< | >>

Luke 13:1

Unganisha maelezo:

Yesu bado akizungumza mbele ya umati wa watu. Hii ni sehemu moja ya hadithi aliyoanza

Habari kwa ujumla:

Katika aya hizi, baadhi ya watu katika umati walimuuliza Yesu swali na anaanza kujibu.

Wakati huo

Msemo huu unajumuisha tukio hili hadi mwisho wa sura ya 12 wakati Yesu alikuwa akifundisha umati wa watu.

ambao damu Pilato kuchanganywa na sadaka yao wenyewe

Hapa 'damu' inahusu kifo cha Wagalilaya. pengine Pilato akaamuru askari wake kuua watu badala ya kufanya hivyo mwenyewe. AT "ambaye askari wa Pilato waliuawa wakati Wagalilaya walipokuwa wakitoa dhabihu."

Unafikiri kwamba hawa Wagalilaya ni wenye dhambi

.......

Hapana nawaaambia

Hapa 'Nawaambia' nasisitiza 'hapana.' AT "Kwa hakika walikuwa si wenye dhambi" au "wewe unakosea kufikiri kwamba mateso yao yanathibitisha kwamba walikuwa wenye dhambi."

Nyinyi nyote mtaangamia kwa njia sawa

"nyinyi nyote pia mtakufa. "Msemo" katika njia hiyo hiyo' ina maana wao watakuwa na uzoefu wa matokeo sawa, si kwamba watakufa kwa njia sawa.

kuangamia

"kupoteza maisha yako " au "kufa"

Luke 13:4

Au wale

Huu ni mfano wa pili wa Yesu kuhusu watu ambao walioteseka. AT "Au kuhusisha wale" au "Fikiria kuhusu wale."

watu kumi na nane

"18 watu"

Siloamu

Hili ni jina la eneo la Yerusalemu

unathani walikuwa wamepotelea dhambini

'Walikuwa wenye dhambi zaidi' au "gani hii kuthibitisha kwamba walikuwa zaidi wenye dhambi?' Yesu anatumia swali kufundisha watu. AT 'sidhani kwamba walikuwa zaidi wenye dhambi

watu wengine

"watu wengine"

Hapana nasema

Hapa "Nasema" inasisitiza "Hapana" AT "Kwa hakika walikuwa si zaidi wenye dhambi" au 'Wewe ni unakosea kufikiri kwamba mateso yao yanathibitisha kwamba walikuwa zaidi wenye dhambi."

angamia

"Kupoteza maisha yako" au "kufa"

Luke 13:6

Habari za jumla

Yesu anaanza kwa kuwaambia mfano kueleza kauli yake ya mwisho, "Lakini kama hamta tubu, nyote pia mtangamia."

Mtu mmoja alikuwa amepanda mti

Mtu alikuwa amepanda mti

Miaka mitatu

3 miaka

Kwani unaleta unaharibifu wa ardhi?

mtu anatumia swali kusisitiza kwamba mti haina maana na mtunza bustan lazima aukata. AT "Je, si basi unaharibu ardhi".

Luke 13:8

kuunganisha maelezo

Yesu alimaliza kusimulia mfano wake. Huu ni mwisho wa sehemu ya hadithi ambayo ilianza

Uache

AT '"usiufanyie kitu chochote huu mti" au " usiukate"

na weka mbolea juu yake

"na weka mbolea kwenye udongo." Mbolea ni kinyesi cha wanyama. Watu huiweka kwenye ardhi kufanya udongo kuwa mzuri kwa mimea na miti.

Ukate

Mtumishi alitoa pendekezo; yeye hakuwa anatoa amri kwa mmiliki. AT "Ngoja niukate" au "Niambie niukata."

Luke 13:10

Habari za jumla

Hii ni sehemu ya pili ya hadithi. aya hizi hutoa taarifa ziliyopita kuhusu mazingira ya sehemu hii ya hadithi na kuhusu mwanamke mlemavu aliyetambulishwa kwenye hadithi

Sasa

neno hili ni alama ya sehemu mpya ya hadithi.

wakati wa Sabato

"Siku ya Sabato." Baadhi ya lugha husema "Sabato" kwa sababu hatujui ambavyo hasa siku ya Sabato ilikuwa.

Tazama, mwanamke alikuwa huko

Neno "tazama" hapa alerts sisi mtu mpya katika hadithi.

Miaka kumi na nane

18 miaka

roho mbaya ya udhaifu

"Roho mbaya kwamba ilimfanya yeye awe dhaifu"

Luke 13:12

Umeponywa udhaifu wako

"Wewe umeponywa kutokana na ugonjwa wako." Kwa kusema hivyo, Yesu alikuwa akifanya na kutokea.

Aliweka mikono yake juu yake

Yeye alimgusa

yeye aliweza kujiinua

AT "yeye alisimama moja kwa moja"

alichukizwa kwa sababu Yesu alikuwa amemponya

AT "alikuwa na hasira kwa sababu Yesu amemponya"

akajibu na kusema

"Alisema" au "alijibu"

Mje na muponywe kisha

AT "njooni basi huponya wakati wa siku hizo sita"

Luke 13:15

Bwana akamjibu

"Bwana alijibu kwa mtawala wa sinagogi"

sio kila mmoja wenu kufungua punda wako ... Sabato?

Yesu anatumia swali kuwafanya wao kufikiri juu ya kitu tayari walijua. AT 'Wewe kufungua punda wako ... Sabato."

Punda au Ng'ombe

Hawa ni wanyama ambao watu kuwatunza kwa kuwapa maji.

Mtoto wa Ibrahimu

AT "uzao wa Ibrahimu"

ambaye Shetani alimfunga

AT "ambaye Shetani alimfanya kilema" au "ambaye Shetani alimfunga kwa ugonjwa huu"

miaka kumi na nane miaka mingi

18 kwa miaka mingi. "neno "mrefu" hapa inasisitiza kuwa miaka kumi na minane ilikuwa muda mrefu sana kwa mwanamke kuteseka. Lugha nyingine wanaweza kuwa na njia nyingine ya kusisitiza hili.

lazima vifungo vyake asifunguliwe ... siku?

Yesu anazungumza kuhusu ugonjwa wa wanawake kana kwamba ni kana kwamba amefungwa. AT "ni haki ya kumfungua yeye kutoka kwa Shetani ... siku" au "ni haki ya kutolewa yeye kutoka vifungo vya ugonjwa huu ... siku."

Luke 13:17

Kama alivyosema mambo hayo

"'Wakati Yesu aliposema mambo hayo"

mambo ya ukufu aliyofanya

"Mambo ya ukufu Yesu alikuwa akifanya"

Luke 13:18

Kuunganisha maelezo

Yesu alianza kwa kuwaambia mfano kwa watu katika sinagogi.

Ufalme wa Mungu unafanana na nini

Yesu anatumia swali kutambulisha kile yeye kitamhusu kufundisha. AT "Mimi nitawaambia ufalme wa Mungu ni kama nini"

nini naweza kuulinganisha nacho

Hii kimsingi ni sawa na swali lililopita. Yesu alitumia hilo kutambulisha nini ataweza kukizungumzia . Baadhi ya lugha wanaweza kutumia yote kwa ujumla, na baadhi kutumia moja tu.

Ni kama mbegu ya Haradali

Mbegu ya haradali ni mbegu ndogo sana ambayo hukua katika mimea kubwa. Kama hii haijulikani, inaweza kutafsiriwa kwa jina la mbegu nyingine kama hiyo au rahisi kama "mbegu ndogo."

na huipanda Bustanini mwake

na hupandwa katika bustani zao. ' Watu hupanda aina ya baadhi ya mbegu kwa kuzitupa ili waweze kuzitawanya katika bustani.

mti mkubwa

Hii ni exaggeration ya kufanya hatua. AT 'kichaka kubwa sana.'

"Ndege wa angani"

"Ndege wa angani." AT "ndege warukao angani" au "ndege".

Luke 13:20

Unganisha maelezo

Yesu alimaliza kuzungumza na watu katika sinagogi. Huu ni mwisho wa sehemu hii ya hadithi.

Kwa nini naweza kulinganisha Ufalme wa Mungu?

Yesu anatumia swali jingine kutambulisha kile yeye ataweza kufundisha.

Ni kama chachu

Kiasi kidogo tu cha chachu kilikua kinahitajika ili kufanya kiasi cha unga kuumuka . Hii inaweza kufanya wazi kama ilivyo katika UDB.

vipimo vitatu vya unga

"kiasi kikubwa cha unga" au kwa muda kwamba utamaduni wako unatumia kwa kupima kiasi kikubwa cha unga.

Luke 13:22

Habari za jumla:

Hii ni sehemu ya nyingine ya hadithi. Yesu anajibu swali kwa kuwaeleza mfano kuhusu kuingia ufalme wa Mungu

Yesu alitembelea kila mji na kijiji ... na kuwafundisha

Hii ni taarifa zilizopita kwamba kutuambia nini Yesu alikuwa akifanya wakati tukio hili lilipotokea.

ni watu wachache tu watakao okolewa

Mungu ataokoa watu wachache tu

pPmbana kuingia kwa kupitia mlango mwembamba

"Fanya Kazi kwa bidii ili kupita njia ya mlango mwembamba." Yesu anazungumza kuhusu ufalme wa Mungu kana kwamba ni nyumba. Yesu anazungumza na kundi, "wewe" alisema katika amri hii ni wingi

Luke 13:25

mmiliki wa nyumba

Hii ina maana ya Mungu. AT "Mungu."

utakuwa umesimama nje

Yesu alikuwa akizungumza na mkuta. mfumo wa "ninyi" ni wingi. Yeye aliwashughulikia wao kama vile hawataingia kwa kupitia mlango katika ufalme

Pound mlango

"Kugonga kwenye mlango"

Ondokeni kwangu

"Nenda mbali na mimi"

watenda maovu

"watu wanaofanya uovu "

Luke 13:28

Unganisha maelezo

Yesu anaendelea kuzungumzia kuingia katika ufalme wa Mungu. Huu ni mwisho wa mazungumzo haya.

lakini nyinyi-nyinyi mulikuwa mutupwe nje

"lakini ninyi wenyewe mulikuwa mutupwe nje." AT "Lakini Mungu atawafukuza nyinyi nje"

Wao watafika

"Watu watakuja"

wa mwisho ni wakwanza

Hii ni kuhusu heshima au umuhimu. AT "baadhi ambao ni muhimu angalau watakuwa muhimu zaidi'"au "baadhi ambaye watu hawata mheshima, Mungu atamheshimu."

Luke 13:31

Kuunganisha Maelezo

Kuunganisha Maelezo Hili ni tukio la lingine katika sehemu hii ya hadithi. Yesu bado yupo njia kuelekea Yerusalemu, wakati baadhi ya Mafarisayo wakizungumza naye kuhusu Herode.

Muda mfupi baadae

'"Muda mfupi baada ya Yesu alipomaliza kusema"

Nenda na ondoka hapa kwa sababu Herode anataka kukuua

Tafsiri hii kama onyo kwa Yesu. Walikuwa wakitoa ushauri aende mahali pengine na kuwa salama.

Herode anataka kukuua

Herode ataagiza watu kumuua Yesu. AT "Herode anataka kupeleka watu wake kuua wewe."

yule mbweha

Yesu alimuita Herode mbweha. Mbweha ni mbwa porini mdogo. Maana inawezekana ni 1) Herode hakuwa tishio kubwa wakati wote 2) Herode alikuwa mdanganyifu

siku ya tatu

Angalia:

haikubaliki kumuua nabii mbali na Yerusalemu

Viongozi wa Wayahudi waliua manabii wengi wa Mungu katika Yerusalemu na Yesu alijua kwamba wangeweza kumuua huko pia. AT "ni katika Jerusalem kwamba viongozi wa Wayahudi huwaua wajumbe wa Mungu."

Luke 13:34

Kuunganisha maelezo:

Yesu alimaliza kukabiliana na Mafarisayo. Hii ni mwisho wa sehemu hii ya hadithi.

Yerusalemu, Yerusalemu

esu anazungumza kana kwamba watu wa Yerusalemu walikuwa huko kumsikiliza. Yesu alisema hii mara mbili ili kuonyesha jinsi alikuwa akisikitisha kwa ajili yao

mnawaua manabii na kuwapiga mawe wale waliotumwa kwenu

Kama itakuwa ni ajabu kushughulikia mji, unaweza kufanya wazi kwamba Yesu kwa kweli akihutubia watu katika mji "wewe watu wanaowaua manabii na kuwapiga mawe wale Mungu aliwatumwa kwenu"

kuwakusanya watoto wako

"Kukusanya watu wako" au 'kukusanya wewe"

kwa jinsi kuku anavyokusanya vifaranga vyake chini ya mbawa zake

Hii inaelezea jinsi kuku inalinda vifaranga wake kutokana na madhara kwa kufunika wao kwa mbawa zake

nyumba yenu imetelekezwa

Hii inaelezea jinsi kuku inalinda vifaranga wake kutokana na madhara kwa kuwafunika wao kwa mbawa zake.Maana inawezekana ni 1) "Mungu amekuacha" au 2) "mji yako ni tupu." Inamaana kwamba Mungu ameacha kulinda watu wa Yerusalemu, hata maadui wanaweza kuwashambulia na kuwafukuza. Huu ni unabii kuhusu jambo ambalo lingetokea hivi karibuni. AT "nyumba yako itakuwa imetelekezwa' au 'Mungu atawaacha ninyi."

huwezi kuniona mimi hadi mtakaposema

"Huwezi kuniona mpaka wakati unakuja wakati utasema" au "wakati mwingine utakaponiona, utasema"

JIna la bwana

Hapa "jina" inahusu nguvu na mamlaka ya Bwana

Luke 14

Luka 14 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Mstari wa 3 unasema, "Yesu aliwauliza wataalam wa sheria ya Kiyahudi na Mafarisayo, 'Je, ni halali kuponya siku ya Sabato, au la?'" Mara nyingi, Mafarisayo walimkasirikia Yesu kwa kuponya siku ya Sabato. Katika kifungu hiki, Yesu awashangaza Mafarisayo. Ilikuwa kawaida Mafarisayo ambao walijaribu kumtega Yesu.

Mabadiliko ya ghafla

Sura hii inabadilika kwa kasi kutoka kwenye mada moja hadi nyingine. Kuna sehemu kadhaa kubwa zilizo na mistari nyingi na mafundisho mengine mafupi yaliyomo katika mstari mmoja.

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Mfano

Luka 14:15-24 ni kama mfano uliopanuliwa. Ufalme wa Mungu unaweza kuwasilishwa kama sikukuu ya harusi au chakula cha jioni. Mfano huu ungeweza kuonyesha kuwa watu wanamkataa Yesu kwa sababu mbalimbali zisizo muhimu na kwa sababu ya hii kukosa kupokea baraka kubwa za Yesu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#kingdomofgod)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Matumizi ya kitendawili

Kitendawili ni taarifa inayoonekana kuwa ya ajabu, ambayo ni kana kwamba inajikana yenyewe, lakini kwa hakika sio ya ajabu. Mfano wa kitendawili katika sura hii: "kwa maana kila mtu atakayejikuza atanyenyekezwa, na yeye atakayejinyenyekeza atainuliwa" (Luka 14:11).

<< | >>

Luke 14:1

Taarifa kwa ujumla

Hii ni sehemu ya pili ya hadithi. Leo ni Sabato na Yesu yuko nyumbani kwa Mfarisayo. Mstari wa 1 huwapa kutumia taarifa za msingi kuhusu mazingira ya hadithi.

kula mkate

"Kula" au "kwa ajili ya chakula." Mkate ilikuwa ni sehemu ya mlo na hutumiwa katika adhabu hii kwa kutaja mlo.

kumuangali yeye kwa karibu

Walitaka kuona kama wangeweza kumshtaki kufanya kitu chochote kibaya.

Tazama, kuna mbele yake alikuwa ni mtu

Neno "tazama" hutahadharisha sisi kwa mtu mpya katika hadithi. lugha yako inaweza kuwa njia ya kufanya hili. kiingeleza anatumia "Kuna mbele yake alikuwa mtu."

alikuwa akisumbuliwa na uvimbe

Uvimbe ni uvimbe unaotokana na ujenzi wa maji hadi katika sehemu za mwili. Baadhi ya lugha inaweza kuwa na jina kwa hali hii. AT "alikuwa akisumbuliwa kwa sababu sehemu ya mwili wake ilikuwa na uvimbe wa maji"

Je, ni halali kumponya... siyo?

"Je, sheria kibali chetu sio kuponya...?

Luke 14:4

Lakini wao wakanyamaza

viongozi wa dini walikataa kujibu swali la Yesu.

Ni nani kati yenu ambaye ana mwana au ng'ombe ... haitakua mara moja kumvuta yeye nje?

Yesu anatumia swali kwa sababu yeye aliwataka kukubali kwamba wao wangemsaidia mtoto wao au ng'ombe, hata siku ya Sabato. Kwa hiyo, ilikuwa haki kwa yaye kuponya watu hata siku ya Sabato. AT "Kama mmoja wenu ana mwana au ng'ombe ... wewe bila ya shaka utamvuta yeye nje mara moja."

Wao hawakuwa na uwezo wa kutoa jibu

Walijua jibu na kwamba Yesu alikuwa sahihi, lakini hawakutaka kusema chochote kuhusu hilo. AT "Walikuwa hawana kitu cha kusema."

Luke 14:7

wale walioalikwa

AT "wale ambao ni viongozi wa Mafarisayo walikuwa wamelikwa kwenye mlo"

viti vya heshima

"Viti kwa ajili ya watu wakuheshimiwa" au"'viti kwa ajili ya watu muhimu"

Wakati wewe umealikwa na mtu

AT "Wakati mtu anapokualika"

kwa sababu mtu anaweza kuwa amemualika ambaye ni wakuheshimiwa zaidi kuliko wewe

AT "kwa sababu mtu anaweza kuwa amamualika mtu ambaye ni muhimu zaidi kuliko wewe"

na kisha kwa aibu

"Basi utajisikia aibu na"

Luke 14:10

Kuunganisha maelezo

Jesus continues speaking to the people at the Pharisee's house.

Unapoalikwa

AT "wakati mtu anakualika kwenye mlo"

mahali pa chini zaidi

"Kiti maana ya mtu angalau muhimu"

kwenda juu zaidi

"sogea kwenye kiti kwaajiri ya watu muhimu zaidi"

Basi utakuwa wakuheshimiwa

AT "Kisha mmoja ambaye aliyekualika wewe atakuheshimu"

ambae anajiinu nafsi yake

"Anajaribu kuangalia muhimu" au "ambaye anachukua nafasi muhimu"

anayejinyenyekeza

"atakuwa ameonyesha kuwa duni" au "atapewa nafasi isiyomuhimu." au "Mungu atakayejinyenyekeza.'

anayejinyenyekeza

"Ambaye amechagua kuangalia isiyo muhimu" au "ambaye amechukua nafasi isiyo muhimu"

atainuliwa

"Itakuwa inaonyesha kuwa muhimu" au "atapewa nafasi muhimu." AT 'Mungu atawainua."

Luke 14:12

kama wao wanaweza

"Kwa sababu wao wanaweza"

na wewe atalipwa

AT "na kwa njia hii kukulipa"

Luke 14:13

Unganisha maelezo

Yesu anaendelea kuzungumza na Mfarisayo aliyemwalika nyumbani kwake.

nawe utakuwa heri

AT"'Mungu atakubariki"

hawawezi kukulipa

AT "hawawezi kuwakaribisha karamu katika kurudi"

maana utalipwa katika ufufuo wa wenye haki

AT "Mungu atakulipa wakati yeye huleta watu wema nyuma ya maisha"

Luke 14:15

Habari za jumla

Mmoja wa watu katika meza anaongea na Yesu na Yesu anajibu kwa kuwaeleza mfano

Heri yeye

mtu alikuwa si akizungumza juu ya mtu fulani. AT "Amebarikiwa mtu yeyote ambaye" au" Jinsi nzuri ni kwa kila mtu. "

yeyeto atakae kula mkate

neno "mkate" hutumika kwa kutaja mlo mzima" AT "ambao kula katika mlo."

Lakini Yesu akamuambia

Yesu akaanza kuelezea mfano

Wakati chakula cha jioni kikiwa kimeandaliwa

AT "Wakati huo kwa chakula cha jioni" au "Wakati chakula cha jioni kikiwa tayari kuanza"

wale walioalikwa

AT "wale waliokuwa wamealikwa"

Luke 14:18

kuunganisha maelezo

Yesu anaendelea kusema mfano wake.

Habari za jumla

Watu wote ambao walialikwa na mtumishi wakampa udhuru kuhusu ni kwanini hawakuweza kuja kwenye karamu

kufanya udhuru

"Kusema kwa nini hawakuweza kuja chakula cha jioni"

Tafadhali udhuru kwangu

"Tafadhali nisamehe' au 'Tafadhali kubali msamaha wangu"

jozi tano za ng'ombe

AT "10 ng'ombe kufanya kazi katika mashamba yangu"

Kuoa mke

tumizi kujieleza ambako ni asili katika lugha yako. Baadhi ya lugha wanaweza kusema "wamezipata ndoa'"au "kuchukuliwa mke."

Luke 14:21

alikasirika

"Akawa na hasira na watu waliokuwa wamealikwa"

mtumishi akasema

Inaweza kuwa muhimu na hali wazi kulisema taarifa ambazo mtumishi alifanya nini bwana amemwagiza. AT "Baada mtumishi akatoka na alifanya hivyo, yeye akarudi na kusema."

nini uliamuli kimekuwa

AT "Nimefanya nini aliamuru"

Luke 14:23

Kuunganisha maelezo

Yesu alimaliza mfano wake.

barabarani na mipakani

Hii ina maana ya barabara na njia nje ya mji. AT "barabara kuu na njia nje ya mji."

kuwatawalia

Aliwadai

ile nyumba yangu inaweza kujaa

"Ili watu wanaweza kuijaza nyumba yangu"

kwa nilicho waambia

Neno "wewe" linamhusu mtumishi.

wale watu

neno hapa kwa "watu" linamaanisha "wanaume watu wazima" na si tu watu kwa ujumla

ambao walikuwa wa kwanza kualikwa

"Ambaye mimi nilimulika wakwanza"

utaonja chakula changu cha jioni

"Kufurahia chakula cha jioni Nimetengeneza"

Luke 14:25

Habari za ujumla

Yesu anaanza kufundisha umati wa watu ambao walikuwa safarini pamoja naye.

Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake mwenyewe ... hawezi kuwa mwanafunzi wangu

Hapa, "chuki' ni exaggeration kuonyesha jinsi muhimu ni kumpenda Yesu zaidi kuliko mtu mwingine. AT "Kama mtu akija kwangu na hanipenda mimi zaidi kuliko yeye anavyompenda baba yake ... hawezi kuwa mwanafunzi wangu" au "Tu kama mtu ananipenda mimi zaidi kuliko yeye anayempenda baba yake mwenyewe ... hawezi kuwa mwanafunzi wangu"

ndiyo, na nafsi yake mwenyewe

"Na hata nafsi yake mwenyewe"

Mtu asipochukua msalaba wake na kunifuata hawezi kuwa mwanafunzi wangu

AT "Kama mtu anataka kuwa mwanafunzi wangu, ni lazima kubeba msalaba wake na kunifuata"

kubeba msalaba wake mwenyewe

Warumi mara nyingi walimfanya mtu kubeba msalaba wake kabla walipomsulubisha. Yesu hamaanishi kila Mkristo ni lazima asulubiwe. Yeye anamaana wao lazima kuwa tayari kuteseka kwa njia yoyote kuwa wanafunzi wake.

Luke 14:28

Maana ni nani katika ninyi, ambaye anatamani kujenga mnara, hatakaa chini kwanza akadirie gharama kwa mahesabu kama ana kile anachohitaji ili kukamilisha hilo?

Yesu anatumia swali kupata watu kufikiri juu ya nini wangeweza kufanya katika hali fulani. AT "Kama mtu alitaka kujenga mnara, bila ya shaka kwanza kukaa chini na kuamua kama alikuwa na fedha za kutosha kukamilisha hilo."

Mnara

Hii inaweza kuwa mnara katika shamba lake. AT "jengo refu" au "sehemu ya juu ya jukwaa."

baada ya kuweka msingi

"Wakati yeye imejenga msingi." AT "wakati yeye anaanza kujenga"

Luke 14:31

Au

Yesu alitumia neno hili kuanzisha hali nyingine ambapo watu kuhesabu gharama kabla ya kufanya uamuzi.

nini mfalme ... si kukaa chini kwanza na kuchukua ushauri ... wanaume?

Yesu anatumia swali jingine kufundisha umati wa watu. AT "unajua kwamba mfalme ... bila kukaa chini kwanza na kuchukua shauri ... wanaume."

kuchukua ushauri

Maana inawezekana ni 1) "kufikiri kwa makini kuhusu" au 2) "kumsikiliza washauri wake."

Kumi elfu ... Ishirini elfu

"10,000...20,000"

Na kama si

"Na kama yeye anatambua kwamba yeye hakuwa na uwezo wa kumshinda mfalme wengine"

yeyote kati yenu ambaye hataacha vyote alivyo navyo, hawezi kuwa mwanafunzi wangu

wale tu kati yenu ambao wataacha vyote walivyo navyo wanaweza kuwa wanafunzi wangu

Kuacha vyote alivyo navyo

Kuacha nyuma vyote alivyo navyo

Luke 14:34

Kuunganisha maelezo

Yesu anamalizia kufundisha umati wa watu.

Chumvi ni nzuri

"Chumvi ni muhimu." Yesu anafundisha somo juu ya wale ambao wanataka kuwa wanafunzi wake.

vipi inaweza kufanyika kuwa chumvi tena?

Yesu anatumia swali kufundisha umati wa watu. AT "hawezi kuwa chumvi tena" au " hakuna anaeweza kuifanya kuwa chumvi tena"

mbolea

Watu kutumia mbolea ku rutubisha bustani na mashamba. Chumvi bila ladha ni haina maana ni haina hata thamani ya kuchanganywa na mbolea. AT "lundo la mbolea' au 'mbolea."

Ni kutupwa mbali

AT "Mtu kuitupilia mbali"

Yeye aliye na masikio ya kusikia, na asikie

AT "Kama una masikio ya kusikia, kusikiliza vizuri" au "Kama unasikia ninachosema, kuwa makini"

Yeye aliye na masikio ya kusikia

"Yeyote anaweza kusikia" au "Mtu anikisikia mimi"

basi naye asikie

"basi naye asikilize vizuri" au "basi naye awe makini kwa kile nisemacho"

Luke 15

Luka 15 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Mfano wa mwana mpotevu

Luka 15:13-32 ni mfano mmoja, unaojulikana kama mfano wa mwana mpotevu. Kuna takwimu tatu katika hadithi. Kwa ujumla inakubaliwa kuwa baba anaonyesha mfano wa Mungu (Baba), mwana mdogo mwenye dhambi anaonyesha mfano ya wale wanaotubu na kuja kwa imani katika Yesu, na mwana yule mkubwa anayejigamba kuwa mwenye haki anaonyesha mfano ya Wafarisayo. Msamaha unaoonyeshwa kwa mwana aliyepotea na mwenye dhambi unakuwa kizuizi kwa mwana mkubwa, na kumfanya kukataa baba. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#forgive)

Dhana maalum katika sura hii

"Wenye dhambi"

Mafarisayo hutaja kundi la watu kuwa "wenye dhambi." Viongozi wa Kiyahudi walidhani watu hawa walikuwa wenye dhambi, lakini kwa kweli viongozi wenyewe walikuwa pia wenye dhambi. Hali hii inaweza kuchukuliwa kama kinaya. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-irony)

<< | >>

Luke 15:1

Habari kwa ujumla

Hii ni sehemu ya pili ya hadithi. Hatujui sehemu ambapo haya yalijir; ni tu siku moja wakati Yesu alikuwa akifundisha.

Sasa

hii ni mwanzo wa sehemu mpya ya hadithi.

Mtu huyu anakaribisha wenye dhambi

"Mtu huyu amaleta wenye dhambi mbele yake" au "Mtu huyu ameshiriki na wenye dhambi"

Mtu huyu

Walikuwa wakizungumza kuhusu Yesu.

hata anakula nao

neno "hata" inaonyesha kwamba wao walidhani ilikuwa mbaya kwamba Yesu kuruhusu wenye dhambi kuja kwake, lakini ilikuwa mbaya zaidi kwamba angeweza kula pamoja nao.

Watoza ushuru wote.

Hii ni kusisitiza kuwa kulikuwa na watu wengi sana. "watoza ushuru wengi"

Luke 15:3

Taarifa kwa ujumla

Yesu anaanza kwa kuwaambia mifano kadhaa. mfano wa kwanza ni kuhusu mtu na kondoo wake.

kwao

Hapa "wao" inamaanisha viongozi wa dini.

Nani kati yenu ... mpaka ampate?

Yesu anatumia swali kuwakumbusha watu kwamba kama yeyote kati yao akipoteza mmoja wa kondoo wake, wataenda kumtafuta. Baadhi ya lugha na njia za kuonyesha kwamba hii ni hali dhahania na si hadithi kuhusu mtu fulani ambaye amepoteza kondoo.

Nani kati yenu, kama ana kondoo mia

Kwakua mfano umeanza na "Nani kati yenu," baadhi ya lugha zingeendeleza mfano katika mtu wa pili. "Tuseme mmoja wenu, kama ana kondoo mia"

mia ... tisini na tisa

tisa "100 ... 99"

Nani kati yenu ... hata waacha... mpaka ampate?

Yesu anatumia swali kuwakumbusha watu kwamba kama mmoja kati yao wamepoteza mmoja wa kondoo zao, wao bila ya shaka huenda kumtafuta. "Kila mtu ... bila ya shaka huondoka ... mpaka ampate." Baadhi ya lugha na njia za kuonyesha kwamba hii ni hali dhahania na si hadithi kuhusu mtu fulani ambaye amepoteza kondoo.

mia ... tisini na tisa

tisa "100 ... 99"

kumlaza mabegani mwake

Hii ilikuwa njia ambayo wachungaji walibeba kondoo. Hii inaweza kusemwa "kumlaza mabegani mwake na kumbeba nyumbani"

Luke 15:6

Wakati anakuja nyumbani

"Wakati mmiliki wa kondoo anakuja nyumbani" au "Wakati umefika nyumbani". Rejea mmiliki wa kondoo kama alivyofanya katika mstari uliopita.

hata hivyo

"katika njia sawa" au "kama mchungaji na marafiki na majirani wangefurahia"

kutakuwa na furaha mbinguni

"kila mtu mbinguni atafurahi"

wenye haki tisini na tisa wasio hitaji kutubu

wenye haki tisini na tisa wasio hitaji kutubu. Yesu hakuwa akisema kwamba kweli kuna watu wenye haki. Anamaanisha watu ambao wanadhani ni wenye haki, ila sio. "Watu 99 ambao wanadhani kwamba wao ni wenye haki na hawana haja ya kutubu."

watu tisini na tisa wenye haki

watu tisini na tisa wenye haki "watu 99 wema"

zaidi ya watu wenye haki tisini na tisa wasio hitaji kutubu.

watu wenye haki tisini na tisa wasio hitaji kutubu Hii haina maana kwamba Mungu hana radhi kwa wale wanaomtii anachukua furaha kubwa ndani yao. Lakini furaha mbinguni kwa wakati mtu anaokolewa kutoka dhambini ni hata furaha zaidi!

hawana haja ya kutubu

Hii haina maana kwamba waumini hawana haja ya kutubu wote wanahitaji kufanya.

Luke 15:8

Kuunganisha kauli:

Yesu anaanza kuwaambia mfano mwingine. Ni kuhusu mwanamke na shilingi kumi.

Au mwanamke gani ... hatawasha taa ... na kutafuta kwa bidii hata aipate?

Yesu anatumia swali kuwakumbusha watu kwamba yeyote kati yao akipoteza safara ya fedha, bila shaka ataanza kuitafuta kwa bidii.

Mwanamke gan.

Hii ni hali dhahania na si hadithi kuhusu mwanamke halisi. Baadhi ya lugha ina njia ya kuonesha hili.

Hata hivyo

"Kwa njia hiyo hiyo" au "Kama vile watu hushangilia pamoja na mwanamke"

mwenye dhambi mmoja anayetubu

"wakati mwenye dhambi mmoja akitubu"

Au mwanamke gani ... hatawasha taa ... na kutafuta kwa bidii hata aipate?

Yesu anatumia swali kuwakumbusha watu kwamba yeyote kati yao akipoteza safara ya fedha, bila shaka ataanza kuitafuta kwa bidii. "Mwanamke yeyote ... bila ya shaka atawasha taa ... na kutafuta kwa bidii hata aipate"

Kama alikua apoteze

Hii ni hali dhahania na si hadithi kuhusu mwanamke halisi. Baadhi ya lugha na njia ya kuonesha hili.

Luke 15:11

Kuunganisha kauli:

Yesu anaanza kuwaambia mfano mwingine. Ni kuhusu kijana ambaye anamuomba baba yake sehemu ya urithi wake.

Mtu mmoja

hii ni utangulizi wa mtu mwingine katika mfano. Baadhi ya lugha zinaweza kusema "Kulikuwa na mtu ambaye"

nipe saiv

mwana alitaka baba yake ampe haraka. Lugha ambazo zina njia ya amri hiyo ina maana kwamba wanataka iyo ifanyike mara moja unapaswa kutumia njia hiyo.

mali ninayo takiwa kurithi

"sehemu ya mali yako kwamba ulipanga kunipa mimi wakati wewe ukifa"

nipe

mwana alitaka baba yake ampe haraka. Lugha ambazo zina njia ya amri hiyo ina maana kwamba wanataka iyo ifanyike mara moja unapaswa kutumia njia hiyo.

sehemu ya mali ambayo inaniangukia mimi

"sehemu ya mali yako kwamba ulipanga kunipa mimi wakati wewe ukifa"

kati yao

"kati ya wanawe wawili"

Luke 15:13

wakakusanya wote aliokua anawadai

"akakusanya vitu vyake" au "kuweka mambo yake katika mfuko wake"

kununua vitu asivyo vihitaji, na kupoteza pesa yake juu ya maisha ya anasa

"kwa kutumia fedha yake yote juu ya vitu asivyo vihitaji"

njaa kali ikaenea nchini kote

"ukame ukatokea huko na nchi nzima haikuwa na chakula cha kutosha"

Sasa

Neno hili limetumika hapa kuadhimisha mapumziko katika hadithi kuu. Hapa Yesu anaeleza jinsi yule mdogo akaenda kutoka kuwa na mengi hadi kuwa katika uhitaji.

kuwa katika mahitaji

"kukosa kile anachokihitaji" au "kutokua na yakutosha"

maisha ya anasa

"kuishi bila kufikiria"

Luke 15:15

Alikwenda

inahusu yule mdogo.

Kujitoa kiajira

"alichukua kazi kwa" au "alianza kufanya kazi kwa ajili ya"

moja wa mwananchi wa nchi ile

"mtu wa nchi hiyo"

kulisha nguruwe

"kuwapa chakula nguruwe wa mtu yule"

angefuraia kula

"alitaka sana kwamba angeweza kula." Ina eleweka kwamba hii ni kwa sababu alikuwa na njaa sana. Hii inaweza kuwa alisema. "alikuwa na njaa ambayo angefurahia kula"

maganda ya maharage

Haya ni maganda ya maharagwe kwamba kukua juu ya mti ....... "maganda ......" au "maganda" au "maganda ya maharage "

Luke 15:17

alipopata ufahamu

msemo huu una maana "akili yake kurejea." "kueleweka vizuri hali yake"

Ni watumishi wangapi wa baba yangu wanaokula chakula cha kutosha

Hii ni sehemu ya mshangao, na si swali. "watumwa wa baba yangu wote wanachakula cha kutosha kula"

kufa kutokana na njaa

Hii pengine si kukisia. Kijana anaweza kweli kuwa amekuwa na njaa.

Nimefanya dhambi dhidi ya mbingun

Wayahudi wakati mwingine walikua wanaepuka kusema neno "Mungu" na walitumia neno "mbinguni" badala yake. "Mimi nimemkosea Mungu,"

Sistahili hata kuitwa mwanao

"Mimi sistahili hata kuitwa mwanao." Hii inaweza kusemwa "Mimi sistahili wewe uniite mwanao"

sistahili tena

"tena sistahili" Ina maana kwamba katika siku za nyuma alikuwa anastahili, lakini sasa hastahili.

nifanye kama mmoja wa watumishi wako

"niajiri kama mfanyakazi wako" au "niajiri nami nitakua mmoja wa wafanya kazi wako" Hili ni ombi, si amri. Na inaweza kuwa na manufaa kwa kuongeza "tafadhali" kama UDB ilivyo fanya.

Luke 15:20

Hivyo mwana mdogo akaondoka na akaja kwa baba yake

"Hivyo aliondoka nchini na kuanza kurudi kwa baba yake." neno "hivyo" linaweka alama tukio hilo kuwa lilichotokea kwa sababu ya kitu kingine kwamba kilichotokea kwanza. Katika kesi hiyo, kijana alikuwa katika haja na aliamua kwenda nyumbani.

aliwaonea huruma

"alikuwa na huruma juu yake" au "alimpenda saana kutoka moyoni mwake"

kumkumbatia na kumbusu

baba alifanya hivyo ili kumuonyesha mwanawe kuwa yeye alimpenda na alikuwa na furaha kwamba mwana alikuwa anakuja nyumbani. Kama watu wanadhani kwamba ni vigumu au ni vibaya kwa mtu kumkumbatia na kumbusu mtoto wake, unaweza kubadilisha na kuweka njia ambayo wanaume katika utamaduni wako huonyesha upendo kwa watoto wao.

mbele yako

Hii ina maana "katika uwepo wako" au "dhidi yeko"

Alipokuwa bado mbali

"Alipokuwa bado mbali sana na nyumbani kwake" au "Alipokuwa bado mbali sana na nyumbani kwa baba yake"

Sistahili kuitwa mwanao

Tazama 15:17

Luke 15:22

joho bora

"vazi bora katika nyumba." "koti bora" au "vazi bora"

weka pete kidoleni

pete ilikuwa ni ishara ya mamlaka ambayo wanaume walivaa kwenye moja ya vidole vyao.

viatu

Watu matajiri wa wakati huo walivaa viatu. Hata hivyo, katika tamaduni nyingi za kisasa itakuwa "viatu."

ndama aliyenona

ndama ni ng'ombe mdogo. Watu huwapa ndama moja ya chakula maalum ili aweze kukua vizuri, na kisha wakati wao humla huyo ndama siku wakitaka kuwa na sikukuu maalum "ndama bora" au "wanyama wadogo tumekuwa tukiwafanya wanenepe"

na kumchinja

maelezo yanaonyesha kuwa walikuwa wanapaswa kupika nyama zinaweza kufanywa safi. "na kumchinja na kuipika."

mwanangu alikuwa amekufa, na sasa yeye yu hai

Mfano huu unamuongelea mwana kuenda kana kwamba alikua amekufa.: "ni kama mwanangu alikuwa amekufa na akawa hai tena" au "nilihisi kama mwanangu alikuwa amekufa, lakini yeye sasa yu hai"

Alikuwa amepotea, na sasa kapatikana

Mfano huu unasema mwana kuwa wamekwenda kana kwamba alikuwa amepotea. "Ni kana kwamba mwanangu alikuwa amepotea na sasa nimemuona au "Mwanangu alikuwa amepotea na amerejea nyumbani"

kumchinja

maelezo yanaonyesha kuwa walikuwa wapike nyama na kuwekwa wazi.: "kumchinja na kumpika"

Luke 15:25

Sasa

Neno hili limetumika hapa kuadhimisha mapumziko katika habari kuu. Hapa Yesu anaanza kwa kuwaambia sehemu mpya ya hadithi kuhusu mwana mkubwa.

mtumishi

neno lililotafsiriwa hapa kama "mtumishi" ni kawaida kutafsiriwa kama "kijana." inaweza kuonyesha kwamba mtumishi alikua mdogo sana.

mambo haya yanaweka yakawa nini

"nini kinatokea"

nje katika shamba

Inasemekana akilua shabani kwasababu alikua anafanya kazi uko.

mwana kondoo alie nona

Tazama 15:22

Luke 15:28

kamwe usivunje sheria yako

"kamwe usiasi sheria yako yoyote" au "daima tii kila kitu ulichoniambia nifanya"

na sikukuu

"kusherehekea"

mwanao

"yule mwana wako" mwana mkubwa alikua anamaanisha ndugu yake kwa njia hii ili kuonyesha jinsi gani anahasira.

aliyekula mali yako pamoja na makahaba

"kupoteza utajiri wako wote juu ya makahaba" au "kutupa mbali fedha yako yote kwa kuwalipa makahaba." Maana inawezekana ni 1) alifikiria hivi ndivyo ndugu yake alitumia fedha au 2) anatumia mafumbo kwa makusudi kukuza dhambi za ndugu yake.

hii miaka mingi

"kwa miaka mingi"

Mimi nimetumika kwa ajili yenu

"Nimefanya kazi kwanguvu kwaajili yako" au "nimefanya kazi kwa bidii kama mtumwa kwa ajili yako"

mwana mbuzi

mwana mbuzi ilikuwa mdogo na sio ghali kuliko ndama aliye nona. "hata mwana mbuzi"

mwana kondoo alie nona

Tazama 15:22

Luke 15:31

baba akamwambia

neno "yake" inahusu mwana mkubwa.

huyu ndugu yako

baba alikuwa anamkumbusha mwana mkubwa kwamba mtu ambaye alikuja nyumbani alikuwa ndugu yake.

Alikua amekufa, na sasa yu hai

Tazama 15:22

Alikua amepotea na sasa amepatikana

Tazama 15:24

Luke 16

Luka 16 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Kusema

Imeandikwa kama Abrahimu alisema "hawatajali hata kama mtu atafufuka kutoka wafu." Hii ni mwelekeo wa ukweli kwamba Yesu atafufuka kutoka kwa wafu na hawatajali ukweli huu.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Sheria na manabii walikuwa wa kutegemewa hadi Yohana alipokuja"

Maneno haya hayamaanishi kanuni za sheria ya Musa zilimalizika wakati wa Yohana Mbatizaji. Ni wazi kutoka kwenye Injili kuwa Yesu aliishi na kuhudumia kulingana na sheria. Kilichobadilika ni ujumbe uliotangazwa. Ndio maana UDB inasema, "Sheria ambazo Mungu alimpa Musa na kile ambacho manabii waliandika zilihuburiwa mpaka Yohana Mbatizaji alifika." (See: Luke 16:16 and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lawofmoses)

<< | >>

Luke 16:1

Kuunganisha kauli:

Yesu anaanza kuwaambia mfano mwingine. Ni kuhusu bwana na wakili wa wadaiwa wake. Hii bado ni sehemu moja ya hadithi na siku hiyo hiyo ambayo ilianza katika

Yesu aliwaambia wanafunzi

sehemu ya mwisho ilikuwa ilivyoagizwa kwa Mafarisayo na waandishi, ingawa wanafunzi wa Yesu walikua sehemu ya umati wakisikiliza.

Kulikuwa na mtu mmoja tajiri

huu ni utangulizi wa mhusika mpya katika mfano.

iliripotiwa kwake

Hii inaweza alisema kama "Watu waliripoti kwa tajiri"

kufuja mali yake

"kutumia mali ya tajiri kipumbavu"

Ni nini hii ninayosikia juu yako?

Tajiri anatumia swali kumkemea wakili. "Nimesikia nini unafanya"

Kutoa hesabu ya usimamizi wako

"panga rekodo zako ili kumkabidhi mtu mwingine" au "Andaa rekodi uliyo andika kuhusu fedha yangu"

Luke 16:3

Nifanye nini ... kazi?

wakili anauliza kwa hiari yake mwenyewe, kama njia ya kupitia upya chaguzi zake.

bwana wangu

Hii ina maana ya mtu tajiri. Wakili hakuwa mtumwa. "mwajiri wangu"

Sina nguvu kuchimba

"Mimi sina nguvu za kulima ardhi" au "Sina uwezo wa kuchimba"

wakati nikiondolewa kutoka kwenye kazi yangu ya usimamizi

hii inaweza kusemwa "wakati nikipoteza kazi yangu ya usimamizi" au "wakati bwana wangu inachukua mbali usimamizi wangu kazi"

Nifanye nini ... kazi?

meneja anauliza kwa hiari yake mwenyewe, kama njia ya kupitia upya chaguzi zake. "Inabidi nifikirie kuhusu nini nitafanya...kazi"

Watu wata nikaribisha katika nyumba zao

Hii ina maana kwamba watu hao watatoa kazi, au mambo mengine ambayo anayahitaji ili aishi.

Luke 16:5

wadeni wa bwana wake

"watu ambao walikuwa katika madeni kwa bwana wake" au "watu ambao wanadaiwa kitu na bwana wake." Katika hadithi hii wadaiwa wanadaiwa mafuta na ngano.

Alisema ... Naye akamwambia

"mdaiwa alisema ... Na wakili akamwambia mdaiwa"

Mapipa mia ya mafuta

Haya yalikuwa yapata lita 3,000 ya mafuta.

mia ... hamsini ... themanini

"100 ... 50 ... 80"

vipimo mia vya ngano

Hii ilikuwa yapata vikapu elfu vya ngano.

Wakili akamwambia mtu mwingine ... Alisema ... Naye akamwambia

"wakili akamwambia mdaiwa mwingine ... mdaiwa alisema ... wakili akamwambia mdaiwa"

Alisema ... Naye akamwambia

"mdaiwa alisema ... Na meneja akamwambia mdaiwa"

mia ... hamsini ... themanini

"100 ... 50 ... 80"

Wakili akamwambia mtu mwingine ... Alisema ... Naye akamwambia

"wakili akamwambia mdaiwa mwingine ... mdaiwa alisema ... wakili akamwambia mdaiwa"

Luke 16:8

Kuunganisha kauli:

Yesu alimaliza mfano huo kuhusu bwana na wakili wa wadaiwa wake. Katika mstari wa 9, Yesu anaendelea kuwafundisha wanafunzi wake.

bwana kisha alimpongeza

maandiko hayaonyeshi jinsi bwana alitambua juu ya matendo ya wakili wake.

alipongeza

"kusifiwa" au "akamsifu" au "kumpitisha "

yeye alikuwa ametenda ......

"alikuwa alitenda vyema" au "Yesu alikuwa amefanya jambo la busara"

Wana wa ulimwengu huu

Hii ina maana ya wale kama meneja wa udhalimu ambao hawajui au kutokujali juu Mungu. "Watu wa dunia hii" au "watu wa kidunia"

Wana wa nuru

Hii inamaanisha watu wenye haki wasio na chakuficha. "wana wa nuru" au "watu waishio kwenye mwanga"

Nina kwambia wewe

"Nina" inasemea Yesu. maneno "nawaambia" yanaweka alama ya mwisho ya hadithi na sasa Yesu anasimulia watu jinsi ya kutumia hadithi kwa maisha yao.

makao ya milele

Hii ina maana ya mbinguni ambako Mungu anaishi.

kujifanyieni marafiki kutokana kwa njia ya fedha isiyo halali

lengo hapa ni juu ya kutumia fedha kusaidia watu wengine, sio kwa njiacambayo utajiri unapatikana kwa uongo.

fedha isiyo ya halali

Inawezekana Maana ni 1) "fedha iliyopatikana kidhuluma" au 2) fedha iliyo patikana kwa mambo ya kidunia.

wanaweza kuwakaribisha

Hii inaweza kutaja 1) Mungu wa mbinguni, ambaye ameridhika kwamba umetumia hela kuwasaidia watu, au 2) marafiki ulio wasaidia na fedha yako.

Luke 16:10

nani atakayewakabidhi na mali za kweli?

Yesu anatumia swali kufundisha watu. "hakuna mtu atakayewakabidhi nyinyi mali ya kweli" au "hakuna mtu nitakupa utajiri wa kweli wa kusimamia"

ambao nitakupa fedha yako mwenyewe?

Yesu anatumia swali hili kufundisha watu. "hakuna mtu atakupa utajiri kwa nafsi yako"

Yeyote aliye mwaminifu

"Watu ambao ni waaminifu." Hii itakuwa ni pamoja na wanawake.

mwaminifu katika jambo dogo

'waaminifu hata kwa mambo madogo. " hakikisha hii haina sauti kama hao sio waaminifu sana.

mwaminifu katika mambo madogo sana

"wasio waadilifu hata katika mambo madogo." Kuhakikisha hii haina sauti kama sio waovu mara nyingi.

fedha isiyo ya halali

Tazama 16:08

mali wa kweli

hii inahusu mali ambayo ni zaidi ya kweli, halisi, au kudumu kuliko fedha ya udhalimu.

Luke 16:13

Taarifa kuu:

Hii ni mapumziko katika mafundisho ya Yesu, kama mstari wa 14 inatuambia taarifa za msingi kuhusu jinsi Mafarisayo wakamdharau Yesu. Katika mstari wa 15, Yesu anaendelea kufundisha na anaitikia kwa Mafarisayo.

Hakuna mtumishi anaweza

"mtumishi hawezi"

atamchukia

"mtumishi chuki"

kujitoa

"kujitolea." Hii ina maana kimsingi ni sawa na "upendo" katika kifungu uliopita.

kumdharau huyu

"kushikilia mmoja katika dharau" au "chukia mwingine"

Huwezi kumtumikia

Yesu alikuwa akizungumza na kundi la watu, hivyo lugha ambazo zina wingi wa "wewe" bila kutumia hiyo.

kutumika

"kuwa mtumwa"

kutumikia mabwana wawili

"kutumikia mabwana wawili tofauti kwa wakati mmoja"

kwa maana ata ... au pengine ata

Vifungu hivi viwili ni vinafanana tofauti kubwa ni kwamba bwana kwanza amechukiwa katika kifungu cha kwanza, lakini bwana wa pili amechukiwa katika kifungu cha pili.

kumdharau

Hii ina maana kimsingi ni sawa na "chuki" katika kifungu kilichopita.

Luke 16:14

Sasa

neno hili lina weka alama ya kuhama kutoka katika taarifa ya awali.

ambao walikuwa wanapenda sana fedha

"aliyependa kuwa na fedha" au "ambaye alikua na tamaa ya fedha"

wao wakamdharau

"Mafarisayo wakamdharau Yesu"

Naye akawaambia

"Na Yesu aliwaambia Mafarisayo"

Nyie mnajihalalisha wenyewe mbele ya watu

"wewe unajaribu kujifanya kuonekana vizuri kwa watu"

Mungu anaijua mioyo yenu

Hapa "mioyo" inahusu tamaa za watu."Mungu anaelewa tamaa yako kweli" au "Mungu anajua nia yako"

Iyo iliyotukuka miongoni mwa watu

hii inaweza semwa kama "Yale mambo ambayo watu wanadhani ni muhimu sana"

ni machukizo mbele za Mungu

"Mungu anachukia" au "ni mambo ambayo Mungu anayachukia"

Taarifa kuu:

Hii ni mapumziko katika mafundisho ya Yesu, kama mstari wa 14 unatuambia taarifa za msingi kuhusu jinsi Mafarisayo wakamdharau Yesu. Katika mstari wa 15, Yesu anaendelea kufundisha na anawajibu Mafarisayo.

Luke 16:16

sheria na manabii

Hii inahusu maneno yote ya Mungu kwamba yalikuwa yameandikwa hadi wakati huo.

Yohana alikuja

Hii ina maana ya Yohana Mbatizaji. "Yohana mbatizaji alikuja"

injili ya ufalme wa Mungu hutangazwa

Hii inaweza semwa kama: "Mimi nafundisha watu kuhusu habari njema ya ufalme wa Mungu"

kila mmoja anajaribu kulazimisha njia yao ndani yake

Hii ina maana ya watu ambao walikuwa wakisikiliza na kukubali mafundisho ya Yesu. "Watu wengi wanafanya kila liwezekanalo kuingia"

ni rahisi zaidi mbingu na dunia kupita, kuliko

"kama unavyo jua kuwa mbingu na ardhi hawezi kupita, unaweza kuwa na uhakika kwamba"

kuliko hata herufi moja ya sheria ikosekane

maneno "herufi moja ya sheria" maana yake ni sehemu ndogo ya barua. Ni inahusu kitu katika sheria ambayo inaweza kuonekana kuwa haina umuhimu saana. "kuliko kwa mtu kuondoa hata undani ndogo ya sheria."

ni rahisi zaidi mbingu na dunia kupita kuliko hata herufi moja ya barua ya sheria kukosekana

Hii inaweza kusemwa kama, "hata herufi ndogo ya barua ya sheria itadumu saana kuliko mbingu na nchi kuwepo"

kuliko hata herufi moja ya barua

"Herufi" ni sehemu ndogo ya barua. Ni inahusu kitu katika sheria ambacho kinaweza kuonekana kuwa hakina umuhimu saana. "kuliko kwa hata undani mdogo wa sheria"

kuwa batili

"mwisho" au "kusitisha kuwepo"

Luke 16:18

Kila mtu amwachaye mkewe

"Anayemwacha mkewe" au "Mtu yeyote anayemtalaka mke wake"

anazini

"ni hatia ya kufanya uzinzi"

naye amwoaye moja

"mtu yeyote anayemwoa mwanamke"

Luke 16:19

Kuunganisha kauli:

Wakati Yesu akiendelea kufundisha watu akaanza kuwaambia mfano. Ni kuhusu tajiri na Lazaro.

Taarifa kuu:

Hii nistari inatoa taarifa kuhusu hadithi. Yesu anaanza kueleza kuhusu tajiri na Lazaro.

ambaye alikuwa amevaa nguo ya zambarau na kitani safi

"ambao walivaa mavazi yaliyo tengenezwa na kitani safi" au "ambao walivaa nguo ghali sana." rangi ya zambarau na kitani safi zilikua nguo ghali sana.

alikua akifurahia kila siku utajiri wake

"kufurahia kula chakula cha gharama kila siku" au "alitumia fedha nyingi na kununua chochote akitakacho"

maskini mmoja jina lake Lazaro, aliwekwa mlangoni pake

Hii inaweza semwakama "Watu walikuwa wamemlaza maskini mmoja jina lake Lazaro kwenye lango lake"

kwenye lango lake

"katika lango la nyumba ya tajiri" au "katika mlango wa kuingia kwenye mali ya tajiri"

kufunikwa na vidonda

"na vidonda yote juu ya mwili wake"

yeye alitamani sana kulishwa na kile kilichoanguka kutoka meza ya tajiri

Hii inaweza semwa kama: "alitamana tajiri ampe makombo ya chakula ambayo atayatuma"

kando na hayo

hii inaonyesha kwamba kile kifuatavyo ni kibaya zaidi kuliko yale ambayo tayari yameelezwa kuhusu Lazaro. "katika nyiongez ya hayo" au "hata"

Mbwa

Wayahudi huchukuliwa mbwa kuwa wanyama wasio safi. Lazaro ni mgonjwa sana na dhaifu hata kufukuza mbwa wasimlambe vidonda vyake.

Luke 16:22

Ikawa kwamba

maneno haya yametumika hapa kuadhimisha tukio katika hadithi. Kama lugha yako ina njia kwa ajili ya kufanya hii, unaweza kufikiria kutumia hapa.

akachukuliwa na malaika

Hii inaweza alisema katika fomu ya kazi. AT: "Malaika wakamchukua mbali"

Upande wa Ibrahamu

Inavyoonekana Ibrahim na Lazaro walikuwa wameketi karibu wakati wa sikukuu mbinguni. Hii ilikuwa ni desturi ya Kigiriki kualika wageni katika karamu. "kukaa karibu na Ibrahimu" au "uketi karibu na Ibrahimu."

na alizikwa

"na watu walimzika"

na katika kuzimu, alipokuwa katika mateso

"naye akaenda kuzimu ambapo alikuwa akiteseka katika maumivu ya kutisha"

Akainua macho yake

"akaangalia juu"

na Lazaro dhidi ya kifua chake

"Lazaro na ameketi karibu na Ibrahimu" au "na Lazaro pamoja naye"

Upande wa Ibrahimu.... dhidi ya kifua chake

Hii inaonyesha kwamba Ibrahimu na Lazaro walikua wameketi karibu, katika utamadunu wa kigiriki.

alizikwa

"Watu walimzika"

katika kuzimu, alipokuwa katika mateso

"alikwenda kuzimu, ambapo aliteseka katika maumivu ya kutisha"

Lazaro dhidi ya kifua chake

"Lazaro ameketi karibu na Ibrahimu" au "Lazaro karibu naye"

Luke 16:24

Naye akasema kwa sauti

"na tajiri aliita na kusema" au "alipiga kelele kwa Ibrahimu"

Baba Ibrahimu

Ibrahimu alikuwa babu wa Wayahudi wote, ikiwa ni pamoja na mtu mmoja tajiri.

nihurumie

"tafadhali nihurumie" au "tafadhali uniwie radhi mimi"

umtume Lazaro

"kwa kumtuma Lazaro" au "na kuwaambia Lazaro kuja kwangu"

achovye ncha ya kidole chake

Hii inaonyesha udogo wa kiasi alichoomba. "aweze kuloanisha ncha ya kidole chake"

Niko kwenye mateso katika moto huu

"Niko kwenye mateso katika moto huu " au "Mimi naumia sana katika moto huu"

alipiga kelele na kusema

"tajiri alilia kwa kusema" au "alipiga kelele kwa Ibrahimu"

Luke 16:25

Mtoto

tajiri alikuwa mmoja wa kizazi cha Ibrahimu.

mambo mema

"mambo mazuri"

katika njia hiyohiyo mambo mabaya

"katika njia hiyohiyo alipokea mambo mabaya" au "vivyo alipata mambo ambayo yalimfanya ateseke"

yeye anatulizwa

"yeye anatulizwa hapa" au "yeye anafuraha hapa"

kwa uchungu

"mateso"

Zaidi ya hayo yote

"kwa kuongeza sababu hii"

shimo kubwa imara limewekwa

Hii inaweza kusemwa kama. "Mungu ameweka bonde kubwa kati ya wewe na sisi"

shimo kubwa

"mwinuko, kina na bonde kubwa" au "kujitenga kubwa" au "bonde kubwa"

wale ambao wanataka kuvuka

"watu wale ambao wanataka kuvuka shimo" au "kama kuna mtu anataka kuvuka"

wenyeji wake walifanya kama

hii inahusu ukweli kwamba wao wote hupokea kitu wakati wao waliishi duniani. Si kusema kwamba kile walikipata mara moja. "wakati alipokuwa hai kupokea"

Zaidi ya hayo yote

"kwa kuongeza sababu hii"

Luke 16:27

kuwa wewe umtume aende nyumbani kwa baba yangu

"kwamba utamwambia Lazaro aende nyumbani kwa baba yangu" au "tafadhali, umtume aende nyumbani kwa baba yangu"

nyumba ya baba yangu

hii inahusu watu katika nyumba. "familia yangu"

ili apate kuwaonya

"ili Lazaro inaweza kuwaonya"

mahali hapa pa mateso

"mahali hapa ambapo sisi kuteseka kwa adhabu" au "mahali hapa ambapo sisi tunateswa maumivu ya kutisha"

kwa hofu kwamba

Hii ina maana yeye hataki hili litokee "ili kwamba wao wasi"

Luke 16:29

Kuunganisha kauli:

Yesu alimaliza kusimulia hadithi kuhusu tajiri na Lazaro.

Wanao Musa na manabii

Ina onyesha kuwa Abraham alikataa kumtuma Lazaro kwa ndugu wa tajiri. Hii inaweza kuwa alisema. "Hapana, sitaweza kufanya ivyo, kwa sababu ya ndugu zenu na yale ambayo Musa na manabii waliandika mda mrefu uliopita"

waache wawasikilize

"ndugu zako lazima wawe makini na Musa na Manabii"

kama mtu aliamua kwenda kwao kutoka katika wafu

"kama mtu ambaye amefariki aliamua kwenda kwao" au "kama mtu ambaye amefariki aliamua kwenda na kuwaonya"

Kama hawata wasikiliza Musa na Manabii

"Kama hawatakuwa makini kwa kilicho andikwa na Musa na manabii"

wala hawataweza kushawishiwa kama mtu angefufuka kutoka wafu

"Wala mtu ambaye atakuja kutoka kwa wafua atakua na uwezo wa kuwashawishi" au "hawatamini hata kama mtu angefufuka kutoka wafu"

Musa na manabii

Hii ina maana ya maandiko yao. "nini Musa na manabii aliandika"

Luke 17

Luka 17 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Katika utakaso wa watu 10 (Luka 17:11-17), lazima kuwe na ufahamu kamili wa muundo wa hadithi hii. Ni hadithi moja iliyounganishwa. Itikio la Msamaria asiyetakasika ni sahihi, lakini itikio la wale wengine haikuwa sahihi na inadhaniwa kuwa walikuwa Wayahudi. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#ungodly)

Dhana maalum katika sura hii

Mifano ya Agano la Kale

Sura hii inatumia mfululizo wa mifano kutoka Agano la Kale. Mifano zote hizi ni wakati ambapo watu hawakujihusisha na Mungu. Kuelewa vizuri maana ya kila mfano itakuwa vigumu bila kuanza kusoma na kuelewa kitabo cha Mwanzo.

Those who read your translation may need help so they can understand what Jesus was teaching here.

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Ingekua afadhali

Hii ni aina maalum ya hali ya fikira. Katika hali hii, badala ya kuzungumza juu ya hali au vitu vingetokea, inatoa ufafanuzi juu ya hali ya baadaye ikiwa hali ya sasa haibadiliki. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-hypo)

Hali ya Kufikiri na Hali ya Uhuishaji

Yesu anatumia takwimu mbili za misemo kwa wakati mmoja katika sura hii. Anashirikisha hali ya kufikiri pamoja na maswali ya uhuishaji kwa sababu jibu sahihi kwa hali ya kufikiri lazima iwe wazi. (See: Luke 17:5-9 and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-rquestion)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Mwana wa Binadamu"

Yesu anajiita mwenyewe kama "Mwana wa Binadamu." Lugha zingine haziwezi kuruhusu mtu kujitaja mwenyewe kama 'mtu wa tatu.'

Matumizi ya kitendawili

Kitendawili ni taarifa inayoonekana kuwa ya ajabu, ambayo ni kana kwamba inajikana yenyewe, lakini kwa hakika sio ya ajabu. Mfano wa kitendawili katika sura hii: "Yeyote anayetaka kupata uhai wake ataupoteza, lakini yeyote anayepoteza uhai wake atauokoa" (Luka 17:33).

<< | >>

Luke 17:1

Kuunganisha kauli:

Yesu anaendelea kufundisha, lakini yeye ataelekeza nia yake kwa wanafunzi wake. Hii bado ni sehemu moja ya hadithi na siku hiyo hiyo ambayo ilianza

Ni hakika kutakuwa na mambo ambayo yanaweza kutufanya kutenda dhambi

"Mambo ambayo huwajaribu watu kutenda dhambi bila ya shaka vitatokea"

kwa mtu huyo atakayevisababisha

"kwa mtu yeyote ambaye husababisha majaribu kuja" au "kwa mtu yeyote ambaye anasababisha watu kujaribiwa"

kama jiwe la kusagia likiwekwa shingoni kwake na angetupwa

Hii inaweza kusemwa: "kama walikuwa waweka jiwe la kusagia shingoni mwake na kumtupa" au "kama mtu alikua awekewe jiwe zito shingoni mwake na kumsukuma"

jiwe la kusagia

Hili ni kubwa sana, jiwe zito la mviringo linalotumika kusaga nafaka za ngano kuwa unga" "jiwe nzito"

hawa wadogo

Hii hapa inahusu watu ambao imani bado ni dhaifu. "Watu hawa ambao imani yao ni ndogo"

na mashaka

Hii ilikua njia ya kumaanisha dhambi za kutokudhamiria. "dhambi"

Itakuwa bora kwa ajili yake kama

Ina maana kwamba adhabu ya mtu huyu kwa kusababisha watu kutenda dhambi itakua mbaya zaidi ya wazima baharini.

kwa ajili yake ... shingo yake ... yeye walikuwa ... anapaswa

Maneno haya rejea wanawake ikiwa ni pamoja na wanaume.

Luke 17:3

Kama ndugu yako akikosa

Hii kauli inaonyesha kwamba tukio hilo pengine litatokea katika siku zijazo.

ndugu yako

"ndugu" hapa limetumika kwa maana ya mtu aliye na imani sawa. "mwamini mwenzetu"

Mkemee

"kumwambia kwanguvu kwamba aliyoyafanya ilikuwa ni makosa" au "msahishe"

Na kama akikukosea mara saba

Hii inaonyesha inaweza isitokee ila kama ikitokea Yesu anawaambia watu wasamehe.

mara saba kwa siku

namba saba katika Biblia ni ishara ya ukamilifu. "mara nyingi katika siku"

Luke 17:5

Habari kwa ujumla:

Kuna mapumziko mafupi katika mafundisho ya Yesu wakati wanafunzi wakizungumza nae. Kisha Yesu anaendelea kufundisha.

Kuongeza imani yetu

"Tafadhali tuongezee imani"

Kama imani yenu ingekuwa kama mbegu ya haradali

"haradali" ni mbegu ndogo sana. Yesu ana maana kwamba hawakuwa na hata kiasi kidogo cha imani.

mti huu wa mkuyu

"mtini" au "mti"

Kungooka na kupandwa baharini

hii inaweza semwa kama: "kujing'oa mwenyewe na kujipanda mwenyewe baharini" au "Chukua mizizi yako nje ya ardhi, na kuweka mizizi yako ndani ya bahari"

ungewatii

"mti ungewatii." Matokeo haya ni masharti. ingeweza kutokea tu kama walikuwa na imani.

mti huu wa mkuyu

Kama aina hii ya mti haufahamiki, inaweza kuwa na manufaa mbadala aina nyingine ya mti. "mtini" au "mti"

Luke 17:7

Lakini ni nani katika yenu, ambaye ana mtumishi

Yesu anauliza kundi kuhukumu hali fulani na mtumishi.

mtumishi anaelima au kutunza kondoo

"mtumishi anaelima shamba lako au analinda kondoo wako"

Je hatambiambia

Yesu anatumia swali kuwafundisha wanafunzi.

jifunge mkanda na unitumikie

"funga nguo yako katika kiuno chako na unitumikie mimi" au "vaa vizuri kisha unitumikie." Watu hufunga nguo zao karibu na viuno vyao ili nguo zao wakati wa kazi zisiwasumbue.

Kisha baada ya hayo

"Kisha baada ya kunitumikia"

Lakini ni nani kati yenu ... atamwambiya ... kaa chini kula '?

Yesu anauliza wanafunzi wake swali kuwasaidia kufikiri juu ya jukumu la mtumishi. Hii inaweza kuwa kauli. "Lakini mtu yeyote kati yenu ... siwezi kusema kwake ... kaa chini kula '"

Je, yeye hatamwambia ... kula na kunywa?

Yesu anatumia swali la pili kueleza jinsi wafuasi wangewa fanyia watumishi. Hii inaweza kuwa kauli. "Naye hakika humwambia ... kula na kunywa '"

Luke 17:9

Kuunganisha kauli:

Yesu alimaliza kufundisha. Huu ni mwisho wa sehemu ya hadithi hii.

Yeye hashukuru

"Yeye hakutaka kuwashukuru" au "Wewe hutashukuru"

mambo yaliyo amuriwa

Hii inaweza kusemwa "Mambo uliyo muagiza afanye"

gani?

"haki?" au "ni hii si kweli?"

wewe pia

Yesu alikuwa akizungumza na wanafunzi wake, hivyo lugha ambazo zina wingi wa "wewe" itakuwa matumizi yake.

yale uliyo amuriwa

Hii inaweza kusemwa kama "kwamba Mungu alikuamuru"

usema

"ukusema kwa Mungu"

Sisi ni watumishi tusiostahili

Hii ni kueleza kuwa wao hawakufanya kitu cha kustaili kusifiwa. "Sisi watumishi wa kawaida" au "Sisi watumishi hatustahili sifa yako"

Hamshukuru mtumishi ... alivyoamuru, je anafanya?

Yesu anatumia swali hili ili kuonyesha jinsi watu wanavyo wafanyia watumishi. Hii inaweza kuwa kauli. "Yeye hakutaka kumshukuru mtumishi ... aliamuru"

Luke 17:11

Habari kwa ujumla:

Hii ni sehemu ya pili ya hadithi. Yesu anaponya watu 10 wa ukoma. Mstari wa 11 na 12 unatoa taarifa za msingi na mazingira ya hadithi.

Ikawa kwamba

maneno haya yametumika hapa kuonyesha mwanzo wa sehemu mpya ya hadithi. Kama lugha yako ina njia kwa ajili ya kufanya hii, unaweza kufikiria kutumia hapa.

na walipokua njiani kuelekea Yerusalemu

"kama Yesu na wanafunzi walipokuwa wakisafiri kwenda Yerusalemu"

huko alikutana na watu kumi wenye ukoma

Hii inaweza semwa kama. "watu kumi wenye ukoma walikutana naye" au "watu kumi waliokuwa na ukoma walikutana naye"

wakapaza sauti zao

kauli hii ina maana kusema kwa sauti kubwa. "wakamwita kwa sauti kubwa" au "wao kuita kwa sauti"

Bwana

neno lililotafsiriwa hapa kama "Bwana" siyo neno la kawaida kwa "Bwana." Hii moja inahusu mtu ambaye ana mamlaka, na si kwa mtu ambaye anamiliki mtu mwingine.

utuhurumie

Walikuwa hasa wanaomba kuponywa. "tafadhali tuonyeshe huruma na utuponye"

alipokuwa akisafiri kwenda Yerusalemu

"kama Yesu na wanafunzi walikuwa wakisafiri kwenda Yerusalemu"

kijiji kimoja

maneno haya haya elezei hicho kijiji.

Nao wakasimama mbali mbali na yeye

Hii ilikuwa ishara ya heshima , kwa sababu wenye ukoma hawakuruhusiwa kukaribia watu wengine.

Luke 17:14

mkajionyeshe kwa makuhani

wenye ukoma walikuwa wanatakiwa kuthibitishwa na makuhani kwamba ukoma wao umepona. "jionyesheni wenyewe kwa makuhani ili waweze kuwachunguza"

Na ikawa kwamba

maneno haya yametumika hapa kuonyesha mwanzo wa sehemu mpya ya hadithi. Kama lugha yako ina njia kwa ajili ya kufanya hii, unaweza kufikiria kutumia hapa.

wakatakasika

Wakati watu waliponywa, wao hawakuwa tena najisi. Hii inaweza kufanywa wazi. "wakawa safi wakati walipo ponywa ukoma wao" au "walikuwa wametibiwa ukoma wao"

alipoona kwamba ameponywa

"kuona kwamba ameponywa" au "alitambua kwamba Yesu aliyemponya"

akarudi

"alirudi Yesu"

kwa sauti kubwa akimtukuza Mungu

"nakumtukuza Mungu kwa sauti kubwa"

Akainama miguuni pa Yesu

"akapiga magoti na kuweka uso wake karibu na miguu ya Yesu." Alifanya hivi kwa kumheshimu Yesu.

Luke 17:17

Kuunganisha kauli:

Huu ni mwisho wa sehemu ya hadithi kuhusu Yesu alivyo ponya wenye ukoma.

Yesu akajibu, akisema

Yesu alijibu kulingana na kile mtu alichokifanya, lakini alikuwa akizungumza na kundi la watu karibu naye. "Basi Yesu akawaambia ule umati"

Je hawakutakasika wote kumi?

Hii ni moja ya maswali matatu. Yesu aliyatumia kwa kuonyesha watu walio karibu naye jinsi alivyo shangazwa na kukatishwa tamaa kwamba moja tu ya watu kumi alirudi kumtukuza Mungu. "Watu kumi waliponywa" au "Mungu akamponya watu kumi"

Wale tisa wako wapi?

"Kwa nini wengine tisa hawakurudi?" Hii inaweza kuwa kauli kwenye. "Watu wengine tisa wanapaswa kurudi, pia"

Hakuna hata mmoja aliyeonekana kurudi ili kumtukuza Mungu, isipokuwa huyu mgeni?

Hii inaweza kuwa kauli kwenye. "Hakuna mtu isipokuwa huyu mgeni akarudi kumtukuza Mungu" au "Mungu akaponya watu kumi, lakini tu huyu mgeni akarudi kumtukuza Mungu"

huyu mgeni

Wasamaria walikuwa hawana mababu Wayahudi na hawakuwa wakimwabudu Mungu kwa njia ile ile ambayo Wayahudi walivyofanya.

imani yako imekuponya

"Kwa sababu ya imani yeko umekuwa vizuri." "Imani" yaweza tajwa kama tendo "Kwa sababu unaamini, umeponywa"

Luke 17:20

Habari kwa ujumla:

Hii ni sehemu ya pili ya hadithi. Hatujui ambapo hili limetokea; ni siku moja wakati Yesu akizungumza na Mafarisayo.

Alipoulizwa na mafarisayo ufalme wa Mungu utakuja lini, Yesu akawajibu akisema,

Hii ​​inaweza semwa kama: "wakamuuliza 'Lini Utawala wa Mungu utakuja?"

Alipoulizwa na Mafarisayo

Huu ni mwanzo wa sehemu mpya ya hadithi. Baadhi ya tafsiri huanza kwa "Siku moja" au "Mara."

Ufalme wa Mungu sio kitu ambacho kinaweza kuonekana

Hii inaweza kusemwa: "Ufalme wa Mungu si kitu ambacho unaweza kuona kwa macho yako" au "Ingawa unanngalia Ufalme wa Mungu, huwezi kuuona"

Utawala wa Mungu uko kati yenu

"Utawala wa Mungu uko hapa" au "Mungu tayari ameanza kutawala kati yenu"

Luke 17:22

Kuunganisha kauli:

Yesu anaanza kuwafundisha wanafunzi wake.

wakati utafika ambapo

"wakati utafika ambapo" au "Labda siku moja"

mtatamani kuona

"wewe utataka sana kuona" au "utakuwa wataka uzoefu"

mojawapo ya siku za Mwana wa Adamu

Hii ina maana ya Utawala wa Mungu. "moja ya siku wakati Mwana wa Adamu atatawala akiwa mfalme"

wala msiwafuate

"na wala kwenda pamoja nao ili kuona"

maana kama vile radi uonekanavyo

"kwa maana kama vile radi ni wazi kwa kila mtu wakati unaonekana na" au "maana kama vile umeme unaonekana ghafla"

ndivyo naye Mwana wa Adamu atakavyokuwa siku yake

hii inahusu ufalme ujao wa Mungu. "itakuwa kana kwamba siku ile Mwana wa Adamu atafika kutawala"

Mwana wa Adamu

Yesu anazungumza juu yake mwenyewe.

lakini huwezi kuiona

"hutaweza kuihisi"

Angalia, pale! Angalia, hapa!

Hii ina maana ya kumtafuta Masihi. "Angalia, Masihi yuko pale! yuko huku!"

maana kama vile radi huangaza

Mwana wa Adamu ajae itakuwa wazi na ghafla, kama muonekano wa radi. "kwa maana kama vile radi ni wazi kwa kila mtu wakati unaonekana na" au "maana kama vile umeme unaonekana ghafla"

Luke 17:25

Lakini kwanza lazimu ateswe

"Lakini kwanza Mwana wa Adamu lazima ateswe." Yesu anazungumza juu yake mwenyewe katika nafsi ya tatu.

na kukataliwa na kizazi hiki

"na kizazi hiki lazima kitamkataa"

Kama ilivyotokea katika siku za Nuhu

"siku za Nuhu" inahusu wakati wa maisha ya Nuhu kabla ya Mungu kuwaadhibu watu wa dunia. "Kama watu walivyokua wakifanya katika siku za Nuhu" au "Kama watu walivyokua wakifanya wakati Nuhu alivyokua akiishi"

hata hivyo itakuwa pia kutokea katika siku za Mwana wa Adamu

"siku za Mwana wa Adamu" inahusu kipindi kabla Mwana wa Adamu atakuja. "Watu watakuwa wakifanya mambo sawa katika siku za Mwana wa Adamu" au "watu watakuwa wakifanya mambo sawa wakati Mwana wa Adamu akikaribia kuja"

Walikula, walikunywa, kuoa, na walipewa katika ndoa

Watu walikuwa wanafanya mambo ya kawaida. Hawakujua au kujali ya kwamba Mungu alikuwa karibu kuwahukumu.

walipewa katika ndoa

hii inaweza semwa kama "Wazazi walikuwa wakiruhusu binti zao kuolewa na wanaume"

Safina

"meli" au "majahazi"

kukataliwa na kizazi hiki

Hii inaweza semwa kama "watu wa kizazi hiki lazima watamkataa"

kuwaangamiza wote

Hii sio pamoja na Nuhu na familia yake waliokuwepo katika safina. "kuharibiwa wale wote ambao hawakuwa katika meli"

Luke 17:28

Ndivyo ilivyokua katika siku za Lutu

"siku za Lutu" inahusu wakati tu kabla ya Mungu haja adhibu miji wa Sodoma na Gomora. "Mfano mwingine ni jinsi ilivyotokea wakati wa Lutu" au "Kama watu walikuwa wakifanya wakati Lutu akiishi"

nao wakala

"watu wa Sodoma walikula"

kulinyesha moto na kiberiti kutoka mbinguni

"moto na kiberiti ukaanguka kutoka mbinguni kama mvua"

kuwaangamiza wote

hii haina ni pamoja Lutu na familia yake. "kuharibiwa wale wote ambao walikaa katika mji"

Luke 17:30

Baada ya namna hiyo itakuwa

"Itakuwa kama hiyo." "Kwa njia hiyo hiyo watu hawtakuwa tayari"

siku ile Mwana wa Adamu atakapofunuliwa

Hii inaweza semwa kama "wakati Mwana wa Adamu ataonekana" au "wakati Mwana wa Adamu anakuja"

usimlete aliye kwenye dari ya nyumba ashuke chini

"yeyote alie juu ya nyumba asishuke" au "mtu akiwa darini kwake, ni lazima asiende chini"

juu ya dari

dari zao zilikuwa bapa na watu kuweza kutembea au kukaa juu zao.

vitu vyake

"mali zake" au "mambo yake"

kurudi

Walikua wasirudi nyumbani kuchukua kitu chochote

Mwana wa Adamu

Yesu anazungumza juu yake mwenyewe. "Mimi, Mwana wa Adamu"

Luke 17:32

Mkumbuke mke wa Lutu

"Kumbuka kile kilichotokea kwa mke wa Lutu!" Hili ni onyo. Yeye aligeuka na kuangalia Sodoma na Mungu akamuadhibu pamoja na watu wa Sodoma. "Msifanye kile mke wa Lutu alichokifanya"

Ye yote anaejaribu kuyaokoa maisha yake atayapoteza

"Watu ambao hujaribu kuokoa maisha yao watayapoteza" au "Yeyote anajaribu kuokoa njia yake za zamani za maisha atapoteza maisha yake"

lakini ye yote atakayeyapoteza maisha yake atayaokoa.

"lakini watu ambao kupoteza maisha yao atawalinda" au "lakini mwenye kukataa njia yake ya zamani ya maisha kuokoa maisha yake"

Luke 17:34

Nawaambia

Kama Yesu anaendelea kuhutubia wanafunzi wake, anasisitiza umuhimu wa nini alichokua akiwaambia.

katika usiku huo

Hii inahusu nini kitatokea kama yeye, Mwana wa Adamu, atakuja wakati wa usiku.

kutakuwa na watu wawili katika kitanda kimoja

mkazo si juu ya watu hawa wawili, lakini juu ya ukweli kwamba baadhi ya watu watachukuliwa na wengine wataachwa.

kitanda

"kochi"

Mmoja atachukuliwa, na mwingine ataachwa

"Mtu mmoja atachukuliwa na mtu mwingine ataachwa." Hii inaweza semwa kama "Mungu atachukua mtu mmoja na kumuacha mwingine" au "Malaika atachukua mmoja na kumuacha mwingine"

Kutakuwa na wanawake wawili wakisaga nafaka pamoja

mkazo si juu ya hawa wanawake wawili au shughuli zao, lakini juu ya ukweli kwamba baadhi ya watu watachukuliwa na wengine wataachwa.

kusaga pamoja

"wakisaga nafaka pamoja"

Luke 17:37

Habari kwa ujumla:

wanafunzi walilomwuliza swali kuhusu mafundisho yake na akawajibu

Ni wapi Bwana?

"Bwana, wapi hii itatokea?"

Ambapo kuna mzoga, ndipo tai hukusanyika pamoja

Inavyoonekana huu ni msemo ukimaanisha "Itakuwa dhahiri" au "Mtaijua ni pale yanapotokea." "Kama tai mkutano inaonyesha kwamba kuna maiti, hivyo mambo hayo kuonyesha kwamba Mwana wa Adamu atakuja"

Tai

Tai ni ndege wakubwa ambao wanaruka pamoja na kula nyama za wanyama waliokufa wakiwapata. Unaweza kuelezea ndege kwa njia hii au kutumia neno kwa ndege wa kawaida wanaofanya hivi.

Luke 18

Luka 18 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Luka 18:6-8 inapaswa kuonekana kama maelezo ya mfano katika 18:1-5.

Dhana maalum katika sura hii

Hakimu asiye na haki

Waamuzi walitakiwa kuendesha haki bila masharti, lakini hakimu huyu hamtendei mwanamke haki. Badala yake, anapaswa kuomba mara nyingi kwa hakimu kufanya jambo linalofaa. Kwa hiyo, hakimu alionyeshwa kama 'asiye na haki." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#justice and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#unjust)

Mafarisayo na watoza ushuru

Luka mara kwa mara anaonyesha kuwa tofauti makundi haya mawili ya watu katika injili yake. Mafarisayo walijiona kuwa ni mifano ya wazi ya wenye haki na kuona watoza ushuru kuwa wenkye dhambi sana, mifano ya wazi ya uovu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#unrighteous and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Mwana wa Binadamu"

Yesu anajiita mwenyewe kama "Mwana wa Binadamu." Lugha zingine haziwezi kuruhusu mtu kujitaja mwenyewe kama 'mtu wa tatu.'

"Aliomba mambo haya juu yake mwenyewe"

Sala ya Mfarisayo kwa hakika haielekezwi kwa Mungu, kwa hiyo kile anachofanya sio maombi. Yeye anadhani anaomba, lakini anazungumza tu ili watu wengine wamsikie na kufikiri kuwa ni mtakatifu.

Maelekezo ya jumla na Maalum

Kuna nyakati ambapo Agano Jipya inatoa maelekezo maalum au amri ambazo zinahusu Wakristo wote. Kwa nyakati nyingine, maelekezo yake ni ya jumla au hata kupita kiasi. Kwa mfano, wakati Yesu anasema, "Uza vitu vyako," hazungumzii na Wakristo wote mahali pote wakati wote, lakini Wakristo wote wanapaswa kukumbuka kwamba wao ni mawakili tu wa kila kitu wanachopokea kutoka kwa Mungu, na anaweza kuwaomba kukitoa wakati wowote. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-hyperbole)

<< | >>

Luke 18:1

Maelezo yanayounganisha"

Yesu anaanza kuwaambia mfano akiendelea kuwafundisha wanafunzi wake. Hii ni sehemu ile ile ya simulizi. Mstari wa 1 unatupa maelezo ya mfano ambao Yesu anataka kuusema.

Kisha

"Kisha Yesu"

Wanapaswa kusali daima wala wasikate tamaa

Sentensi hizi mbili zina maana sawa ambayo Yesu aliitumia ili kusisitiza. Lugha zingine zina namna tofauti za kusisitiza. "Daima muendelee kuomba."

akasema

Hii pia inaweza kuanza kwenye sentensi mpya "Akasema"

Kulikuwa na hakimu katika mji fulani

Neno "fulani" imetumika kuonyesha kuwa hii ilitokea, lakini bila kumuonyesha hakimu au mji.

Kuogopa

Ogopa

Haeshimu watu

"Hajali watu"

Luke 18:3

Sasa kulikuwa na mjane

Yesu alitumia neno hili kumtambulisha mtu mwingine kwenye simulizi.

Mjane

Ni mwanamke ambaye mume wake amekufa. Watu waliomsikiliza Yesu watafikiri kuwa ni mtu ambaye hamna mtu wa kumlinda kutoka kwa wale wanaotaka kumuumiza.

Alimwendea mara nyingi

Neno "yeye" linamaanisha hakimu.

Nisaidie kupata haki dhidi

"waadhibu" au "nisaidie"

Mpinzani wangu

"adui yangu" au "mtu anayejaribu kuniumiza." Huyu ni mpinzani katika mabo ya sheria. Hipo wazi kuwa mwanamke anamshitaki yule mtu au yule mtu anamshitaki mwanamke.

Kumwogopa Mungu

"ogopa Mungu"

Mtu

Hii inamaanisha "watu" kwa ujumla.

Ananisababishia matatizo

"Ananisumbua"

Asinichoshe

"asije akanisumbua"

Kwa kunijia mara kwa mara

"kwa kuja kwangu mara kwa mara"

Luke 18:6

Taarifa ya jumla:

Yesu anamaliza kuwaambia mfano wake na anatoa maelezo kwa wanafunzi wake.

Sikiliza alivyosema huyu hakimu mmbaya

"Fikiri jinsi alivyosema huyu hakimu mmbaya.: Tafsiri kwa namna ambayo watu wataelewa kwamba Yesu tayari aliwaambia alichokisema jaji.

Sasa

Hili neno linaonyesha kuwa Yesu alimaliza kutoa mfano na akaanza kutoa maana yake.

Mungu pia hataleta... usiku?

Yesu alitumia swali kuwafundisha wanafunzi wale.

Wateule wake

"Watu aliowachagua"

Hatakuwa mvumilivu kwao?

Yesu alitumia swali kuwafundisha wanafunzi wake.

Mwana wa Adamu

Yesu alikuwa anajizungumzia mwenyewe.

Atakuta imani duniani?

Dhumuni la mfano huu ni kuwatia moyo wanafunzi wake waendelee kuamini na kuomba. Yesu hapa anatumia swali lingine anayotegemea jibu hasi. "Lakini najua mimi, Mwana wa Adamu, nikirejea, nitawakuta watu wasioniamini."

Luke 18:9

Taarifa ya jumla:

Yesu anaanza kuwaambia mfano mwingine kwa watu wengine waliojiona kuwa wenye haki.

Ndipo yeye

"Ndipo Yesu"

Baadhi

"Baadhi ya watu"

Ambao walijiona wenyewe kuwa wenye haki

"waliokuwa na haki wenyewe" au "waliodhani kuwa wana haki"

kuwadharau

"Kutothamini" au "kudhani kuwa ni bora zaidi ya"

Hekaluni

"kwenye eneo la hekalu"

Luke 18:11

Mfarisayo akasimama, akasali mambo haya juu yake mwenyewe

Maana kwenye maneno ya Kigiriki haipo wazi. inaweza kuwa na maana 1) "Mfarisayo alisimama akaomba juu yake mwenyewe kwa njia hii" au 2) Mfarisayo alisimama pekeyake na akasali."

Majambazi

Jambazi ni mtu anayeiba vitu kwa kumlazimisha mtu ampe au kwa kumtishia kwa nguvu.

Ninayopata

"Ninayopokea"

Luke 18:13

Maelezo yanayounganisha:

Yesu alimaliza kuwaambia mfano. kwenye mstari wa 14, alitoa maelezo kuhusu maana ya mfano huo.

Akainua macho yake juu

"Akaangalia mbinguni" au "akaanalia mbele"

Akapiga kifua chake

Hii ni ishara ya nje ya masikitiko makuu, na kuonyesha namna huyu mtu anavyotubu na unyenyekevu.

Mungu nirehemu mimi, mwenye dhambi

Mungu nakuomba nirehemu mimi, japokuwa ni mtenda dhambi" Mungu, nakuomba unirehemu mimi. Ni mtenda dhambi"

Huyu mtu alirudi nyumbani akiwa amehesabiwa haki.

"Mungu alimsamehe yule mtoza ushuru"

Kuliko yule mwingine

"Kuliko yule mtu mwingine" au "na sio yule mtu mwingine." ' Lakini Mungu hakumsamehe Mfarisayo"

Kwa sabau kila mtu atakayejikweza

Kwenye sentensi hii, Yesu anahama kwenye simulizi na kutoa maelezo ya simulizi.

Atashushwa

"Mungu atamshusha"

Atakwezwa

"Mungu atampa heshima"

Luke 18:15

Maelezo ya kuunganisha:

Hili ni tukio linalofuata kwenye sehemu ya simulizi inayoanza Yesu anawakaribisha watoto na anazungumza nao.

Akawagusa, lakini

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi tofauti. "akawagusa. Lakini"

Wakawazuia

"Wanafunzi walijaribu kuwakataza wazazi wasiwalete watoto kwa Yesu"

waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie

Hizi sentensi mbili zina maana inayofanana na zimewekwa pamoja ili kutia msisistizo. Lugha nyingine zinasisitiza kwa namna tofauti. "Mnatakiwa muwaache watoto wadogo waje kwangu."

Ni wa kwao

"Ni wa watu waliokama hawa watoto"

Amini nawaambia

"Hakika nawaambia." Yesu alitumia maelezo haya kusisitiza umuhimu wa alichokuwa anataka kukisema.

mtu yeyote asiyeupokea Ufalme wa Mungu kama mtoto ni dhahiri hataingia

Mungu anataka watu wapokee ufalme wake kwa kuamini na unyenyekevu. "Yeyote anayetaka kuingia kwenye ufalme wa Munguataupokea kwa kuamini na unyenyekevu kama mtoto mdogo."

Luke 18:18

Maelezo yanayounganisha:

Hii ni tukio linalofuata kwenye sehemu ya simulizi inayoanza. Yesu akaanza kuongea na kiongozi kuhusu kuingia katika ufalme wa Mungu.

Nifanye nini

"Ni kitu gani natakiwa kufanya" au "Ni kipi kinahitajika kwangu"

Kurithi

"kuwa mmiliki halali wa." Hii ina maanisha mali ya mtu aliyekufa. Luka anatumia neno hili kuonyesha kuwa mtawala anafahamu kuwa uzima wa milele hauwezi kuuchuma, na sio kila mtu ataishi milele.

Hakuna mtu aliye mwema, ila Mungu peke yake

"Hakuna mtu aliye mwema kabisa. Mungu pekee ndo mwema"

Usiue

"Usifanye mauaji"

Mambo haya yote

"Amri zote hizi"

Luke 18:22

Yesu aliposikia hayo

"Yesu aliposikia yule mtu akisema hayo"

Akamwambia

"akamjibu"

Umepungukiwa jambo moja

"Bado unatakiwa kufanya jambo moja" au "Kuna jambo moja bado hujalifanya"

Uza vyote ulivyonavyo

"Uza mali zako zote" au "uza vyote unavyomiliki"

Wagawie masikini

"Wape hizo pesa masikini"

Utakuwa na hazina mbinguni

"Utakuwa na baraka za Mungu mbinguni"

Luke 18:24

Kisha Yesu akamwona alivyohuzunika sana

Kifungu hiki hakipo kwenye maneno mengi ya Kigiriki na mara kadhaa huondolewa kwenye tafsiri za kiingereza.

Ngamia kupita katika tundu la sindano

Haiwezekani ngamia kuenea katika tundu la sindano. Kwa hiyo Yesu alitumia mafumbo kuonyesha ni jinsi gani ilivyo ngumu kabisa kwa tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.

Tundu la sindano

Tundu la sindano ni shimo katika sindano ya kushonea ambapo uzi hupita.

Luke 18:26

Waliosikia wakasema

"Watu waliomsikiliza Yesu wakasema"

Je nani atakayeokoka?

Inawezekana kuwa walikuwa wanataka jibu. Lakini ni dhahiri kwamba walitumia swali kuonyesha mshangao wao kwa alichokisema Yesu. "Hivyo hakuna atakayeokoka na dhambi" au "Hivyo Mungu hatamuokoa hata mmoja"

Yanawezekana kwa Mungu

"inawezekana kwa Mungu kufanya"

Luke 18:28

Maelezo yanayounganisha

Huu ni mwisho wa mazungumzo kuhusu kuingia kwenye ufalme wa Mungu.

Kila kitu kilicho chetu

"utajiri wetu wote" au "Mali zetu zote"

Amini, nawaambia

Yesu anatumia maelezo haya kuonyesha umuhimu wa kile anachotaka kukisema.

Hakuna mtu aliyeacha....... ambaye hatapokea

"kila aliyeacha... atapokea"

Na katika ulimwengu ujao, uzima wa milele

"na pia uzima wa milele katika ulimwengu ujao"

Luke 18:31

Maelezo yanayounganisha:

Hii ni sehemu inayofuata ya sehemu ya simulizi inayoanza Yesu haongei tuu na wanafunzi wake tuu.

Tazama

Inaonyesha umuhimu wa mabadiliko katika huduma ya Yesu alivyokuwa akienda Yerusalemu kwa mara ya mwisho.

Yaliyoandikwa na manabii

"ambayo manabii waliandika"

Manabii

Hii inamaanisha Manabii wa Agano la kale.

Mwana wa Adamu

Yesu alikuwa anajielezea mwenyewe kama "mwana wa Adamu" na akatumia "yeye" kujielezea mwenyewe.

Yatatimizwa

"yatatokea" au "yatatimia"

Atatiwa mikononi mwa Mataifa

"Viongozi wa Kiyahudi watamkabidhi kwa Mataifa"

watamtendea dhihaka na jeuri, na kutemewa mate

"watamdhihaki, watamtendea vibaya na kumtemea mate"

Siku ya tatu

Hii inaelezea siku ya tatu baada ya kufufuka. Japokuwa wanafunzi wake hawakumuelewa, hivyo ni vizuri kutokuongeza maelezo haya unapotafsiri mstari huu.

Luke 18:34

Maelezo ya jumla:

Mstari huu sio sehemu ya simulizi lakini ni mawazo kuhusu sehemu ya simulizi hii.

Hawakuelewa mambo haya

"Hawakuelewa kabisa mambo haya"

Mambo haya

Hii inaelezea namna ambavyo Yesu atateseka na kufa Yerusalemu, na atafufuka toka kwa wafu.

Neno hili lilikuwa limefichwa kwao

"Mungu aliwafanya wasielewe maana ya kile alichokuwa akiwaambia"

Mambo ambayo aliyasema

"Mambo ambayo Yesu aliyasema"

Luke 18:35

Taarifa ya jumla

Hii ni sehemu nyingine ya simulizi. Yesu anamponya kipofu alipokuwa anakaribia Yeriko. Mistari hii inatupa historia kuhusu simulizi hii.

Ikawa

Neno hili linatumika kuonyesha mwanzo wa simulizi mpya.

Alipokaribia

"Alipokuwa karibu"

Mtu mmoja kipofu alikuwa ameketi

"kulikuwa na mtu kipofu ameketi" Hapa "mmoja" inaonyesha kuwa mtu huyu alikuwa wa muhimu katika simulizi hii lakini Luka hakutaja jina lale.

Akiomba, na akasikia

"Aliomba. aliposikia"

Wakamwambia

"Makutano wakamwambia kipofu"

Yesu wa Nazareti

Yeso toka mji wa Nazareti uliopo Galilaya.

Anapiata

"Alikuwa akimpita"

Luke 18:38

Hivyo

Neno hili linaweka alama ya tukio limetokea kwa sababu kitu fulani kilitokea kwanza. Kwa hivyo makutano walimwambia kipofu kuwa Yesu anapita.

Akalia kwa sauti

"akaita kwa sauti" au "akapiga kelele"

Mwana wa Daudi

Yesu alikuwa uzao wa Daudi, Mfalme muhimu kwa Israeli.

Nihurumie

"nionee huruma" au "nihurumie"

Wale

"watu"

Anyamaze

"awe kimya" au "asipige kelele"

Akazidi kulia kwa sauti

Hii inaweza kumaanisha alilia kwa sauti zaidi au alilia zaidi kwa kusisitiza.

Luke 18:40

Kwamba mtu yule aletwe kwake

"watu wamlete kipofu kwake"

nataka kuona

aweze kuona tena

Luke 18:42

Imani yako imekuponya

"Nimekuponya kwa sababu umeniamini"

Akamfuata

"Akaanza kumfuata"

Akamtukuza Mungu

"Akampa Mungu utukufu" au "Akamsifu Mungu"

Luke 19

Luka 19 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Luka 19:11-27 ni mfano mmoja. Mfano huu unawafundisha Waumini jinsi ya kuishi katika Ufalme wa Mungu utakapokuja. Wasikilizaji wa Yesu waliamini kimakosa kwamba ufalme huo ungeonekana haraka sana. Ingawa ufalme unaweza kuonekana wakati wowote, maneno haya hayana maana ya kusema ufalme utatokea leo au kesho, lakini itawezekana. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#kingdomofgod)

Dhana maalum katika sura hii

"Mwenye dhambi"

Mafarisayo hutaja kundi la watu kuwa "wenye dhambi." Viongozi wa Kiyahudi walidhani watu hawa walikuwa wenye dhambi, lakini kwa kweli viongozi wenyewe walikuwa pia wenye dhambi. Hali hii inaweza kuchukuliwa kama kinaya. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-irony)

Usimamizi

Ingawa neno hili haitumiwi katika sura hii, ni neno kubwa katika mafundisho haya. Usimamazi ni kuwa mwaminifu katika vitu umepewa kwa kuchungu. Mungu anatarajia kila mtu kutumia vipaji alivyompa. Hii sio tu vipaji au uwezo ambao Mungu amempa mwanadamu, lakini maisha ya mtu anayoyaishi katika matarajio ya uzima wa milele. Mungu pia anatarajia watu kuishi katika matarajio ya kurudi kwa Yesu.

Mwana-punda

Jinsi ambavyo Yesu aliingia Yerusalemu, akiwa amepanda mnyama, ilikuwa sawa na vile ambavyo mfalme angeingia katika mji baada ya ushindi mkubwa. Na kwa wafalme wa Israeli, ilikuwa desturi kupanda punda badala ya farasi. Mathayo, Marko, Luka, na Yohana wote waliandika juu ya tukio hili, lakini hawakuandika maelezo sawa. Mathayo aliandika kuhusu kuwepo kwa punda na mwana-punda, lakini haijulikani ni yupi ambaye Yesu alipanda. Ni bora kutafsiri kila moja ya vifungu hivi kama inavyoonekana katika ULB bila kujaribu kuwafanya wote kusema jambo sawa. (Tazama:Mathayo 21:1-7 na Yohana 12:14-15)

Kutandaza mavazi na matawi

Hii ilikuwa njia ya kumheshimu mfalme.

"[Yesu] akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza"

Imeandikwa kama Yesu alisafisha hekalu kwa kufukuza wafanyabiashara wasio watu wa Mungu kutoka hekaluni. Tukio hili linaonyesha mamlaka ambayo Yesu alikuwa nayo juu ya hekalu na taifa la Israeli. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#clean and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#ungodly)

<< | >>

Luke 19:1

Taarifa ya jumla

Hii ni sehemu iliyofuata ya simulizi. Zakayo anatambulishwa kwenye simulizi. mstari wa kwanza unaonyesha historia ya safari ya Yesu.

Tazama kulikuwa na mtu pale

Neno "tazama" linatuonyesha mtu mpya kwenye simulizi. Lugha yako inaweza kuwa na na njia ya kufanya hivi. "Kulikuwa na mtu ambaye alikuwa"

Alikuwa mkuu wa watoza ushuru na alikuwa tajiri.

Hii ni historia ya Zakayo.

Luke 19:3

Alijaribu

"Zakayo alijaribu"

Kwa sababu alikuwa mfupi wa kimo

"kwa kuwa alikuwa mfupi"

Mti wa mkuyu

"Mti wa mkuyu." unazalisha matunda madogo ya duara yenye sentimita zipatazo 2.5.

Luke 19:5

Mahali

"kwenye mtui" au "alipokuwa Zakaria"

Alikwenda kumtembelea mtu mwenye dhambi

"Yesu alikwenda kwenye nyumba ya mwenye dhambi kumtembelea"

Mwenye dhambi

"mwenye dhambi hasa"

Luke 19:8

Bwana

Hii inamzungumzia Yesu

Wokovu umekuja katika nyumba hii

"Mungu ameokoa nyumba hii"

Nyumba hii

neno "nyumba" inamaanisha watu waishio kwenye nyumba hiyo au familia.

Yeye pia

"huyu mtu pia" au "Zakayo pia"

Mwana wa Ibrahimu

Inamaanisha 1)"kizazi cha Ibrahimu" na 2)"mtu aliyekuwa na imani kama ya Ibrahimu."

Watu waliopotea

"watu waliokua mbali na Mungu" au "wale ambao kutokana na dhambi wako mbali na Mungu"

Luke 19:11

Taarifa ya jumla

Yesu alianza kuwaambia makutano mfano. mstari wa kumi na moja unaonyesha historia kwa nini Yesu aliwaambia mfano huo.

kwamba ufalme wa Mungu ulikuwa karibu kuonekana mara moja.

"kwamba Yesu ataanza kumiliki maramoja kwenye ufalme wa Mungu"

Ofisa mmoja

"Mtu mmoja ambaye alikuwa mmoja wa viongozi" au "mtu mmoja toka kwenye familia ya muhimu." "Mtu wa muhimu"

Kupokea ufalme

Hii ni picha ya mfalme mdogo kumwendea mfalme mkubwa. Mfalme mkubwa atampa mfalme mdogo mamlaka ya kuongoza nchi yake mwenyewe.

Luke 19:13

Aliwaita

Ofisa aliwaita

Akawapa mafungu kumi

"akawapa kila mtu fungu moja"

Mafungu kumi

Fungu ni gramu 600. kila fungu linathamani ya malipo ya miezi minne ya mtu, "Sarafu kumi" au "kiasi kikubwa cha pesa"

Fanya biashara

"fanya biashara na pesa hizi" au "tumia hizi pesa ili upate zaidi"

Wananchi wake

Watu wa nchi yake"

Mabalozi

"wawakilishi" au "wajumbe"

Ikawa

Neno hili limetumika kuonyesha umuhimu wa tukio kwenye simulizi. Kama lugha yako ina namna nyingine ya kufanya hivi unaweza ukaitumia hapa.

Baada ya kuupokea ufalme

"Baada ya kuwa Mfalme"

Waitwe kwake

"kwenda kwake"

Mmetengeneza faida kiasi gani

"ni pesa kiasi gani waliipata"

Luke 19:16

Wa kwanza

"Mtumishi wa kwanza"

Akaja mbele yake

"Akaja mbele ya Afisa"

Umefanya vyema

"wewe umefanya vyema" Lugha yako inaweza kutafsiri kifungu hiki kwamba mwajiri anatumia kuonyesha kiridhika, kama vile "kazi nzuri."

Luke 19:18

Fungu lako, Bwana, limefanya mafungu matano.

"Bwana kwa pesa ulizonipa, nimezalisha mara tano"

Chukua mamlaka juu ya miji mitano

"Utakuwa na mamlaka juu ya miji mitano"

Luke 19:20

Mtu mkali

'Mtu wakali' au 'mtu ambaye anatarajia mengi toka kwa watumishi wake'

Unachukua kile usichokiweka

Ni fumbo linaloelezea mtu mkorofi. "unaondoa kitu asichokiweka" au "unachukua kitu ambacho sio chako."

Kuvuna kile usichopanda

"Kuvuna usichokipanda." Mtumishi alikuwa anamfananisha bwana wake na mkulima anayechukua chakula ambacho mtu mwingine alikipanda.

Kuvuna

"kukusanya" au "kuweka"

Luke 19:22

Kwa maneno yako mwenyewe

"Kutokana na ulichokisema"

Kwamba mimi ni mtu mbaya, nachukua

Afisa alirudia maneno aliyoyasema mtumishi juu yake. Hakusema kuwa ilikuwa kweli.

Mtu mkali

"mtu mkorofi"

Kwa nini hukuweka pesa yangu...... faida?

Afisa alitumia swali ili kumkemea Mtumishi dhalimu. "Ungeweka pesa yangu..... faida."

Weka pesa yangu benki

"Kopesha pesa zangu benki" Tamaduni ambazo hazina benki zaweka kutafsiri kuwa "Acha mtu aazime pesa zangu."

Benki

Benki ni biashara salama ya kuweka pesa za watu. Benki huwakopesha watu pesa kwa faida. Hivyo inalipa pesa ya ziada au faida kwa watu wanaoweka pesa zao benki.

Nitakusanya na faida

"Ningekusanya kiasi hicho cha fedha pamoja na faida iliyopatikana" au "ningepata faida"

Faida

Faida ni pesa ambayo benki humlipa mtu anayeweka pesa zake katika benki.

Luke 19:24

Afisa

Afisa aliyekujakuwa mfalme. Tafsiri hivi kwa maneno ambayo yataeleweka kwa wasomaji.

Waliokuwa wamesimama hapo

"Watu waliokua wamesimama karibu nao"

Luke 19:26

Taarifa ya jumla

Yesu amemaliza kuwaambia mfano wake na sasa anatoa mawazo juu ya makutano nyumbani kwa Zakayo.

Nawaambia

Hii ilikuwa kauli ya mfalme. Watafsiri wengine wanaweza kutaka kuanza mstari huu kwa kusema "Na mfalme akajibu, 'Nawaambia ninyi" au Lakini mfalme akasema, Namwaambia hivi"

Kila aliyenacho

"kila mtu atakayetumia vizuri alichopewa" au "kila mtu atakayetumia vizuri vitu nilivyompa"

Atapewa zaidi

"Ntampa zaidi"

Toka kwake ambaye hana

"Toka kwa mtu ambaye hatumii vizuri kile nilichompa"

Kitaondolewa

"Nitakichukua kutoka kwake"

Hawa adui zangu

Kwa kuwa adui zake hawakuwepo pale, lugha nyingine zawezasema "wale adui zangu."

Luke 19:28

Maelezo yanayounganisha

Huu ni mwisho wa simulizi kuhusu Zakaria. Mstari huu unaelezea aliyoyafanya Yesu baada ya simulizi hii.

Alipomaliza kusema maneno haya

"Yesu alipomaliza kusema maneno haya"

Kwenda Yerusalemu

Yerusalemu ilikuwa kama mita 975 juu ya Yeriko.

Luke 19:29

Maelezo ya Jumla

Hii ni sehemu nyingine ya simulizi. Yesu anakaribia Yerusalemu.

Ikawa

Aya hii imetumika kuonyesha mwanzo wa simulizi mpya. Kama lungha yako ina njia nyingine ya kusema hivi unaweza ukatumia hivyo.

Alipofika karibu

Neno "yeye" linamaanisha Yesu. Wanafunzi wake walisafiri pamoja naye.

Bethfage

Bethfage kilikuwa kijiji kwenye mlima wa Mizeituni, ambayo imepita katikati ya bonde la Kidron toka Yerusalemu.

Mlima ulioitwa Mizeituni

"Mlima ulioitwa Mlima wa Mizeituni" au Mlima ulioitwa "mlima wa mti wa Mizeituni"

Mwanapunda

"Punda mdogo" au "myama mdogo wa kumuendesha"

Ambaye hajapandwa bado

"ambae hamna mtu aliyemtumia"

Luke 19:32

Wale waliotumwa

"Wale waliotumwa na Yesu" au "Wanafunzi wawili waliotumwa na Yesu"

Walitandika mavazi yao juu ya mwanapunda

"waliweka nguo zao juu ya mwanapunda." Mavazi ni nguo. Hapa inamaanisha mavazi ya nje au nguo.

Walitandaza mavazi yapo

"watu walitandaza mavazi yao" au "wengine walitandaza mavazi yao." Hii ni ishara ya kuonyesha heshima kwa mtu fulani.

Luke 19:37

Alipokuwa nateremka katibu

"Yesu alipokaribia" au "Yesu alipokuwa anakaribia." Wanafunzi wa Yesu walikuwa wakisafiri pamoja naye.

Mambo makubwa waliyoyaona

"Mambo makubwa waliyoyaona yakifanywa na Yesu"

Amebarikiwa Mfalme

Walisema haya kuhusu Yesu

Kwa jina la Bwana

Hapa "jina" linaelezea nguvu na mamlaka. Pia "Bwana" linamaanisha Mungu

Utukufu juu

"Acha kila mtu amtukuze yeye aliye juu sana" au "acha kila mtu amsifu aliye juu"

Luke 19:39

Wanyamazishe wanafunzi wako

"waambie wanafunzi wako waache kufanya mambo haya"

Nawaambieni

Yesu alisema hivi kuonyesha msisitizo wa alichotaka kukisema baadae.

Hawa wakinyamaza

Tafsiri zingine zinahitaji kuweka wazi kile ambacho Yesu alikuwa ikimaanisha pale aliposema 'Hapana, mimi sitawakemea, kwa maana hwa watu wakikaa kimya.'

Mawe yatapaza sauti

"Mawe yatasifu"

Luke 19:41

Kukaribia

"Kusogelea" au "kuwa karibu"

Mji

Hii inamaanisha Yerusalemu.

Aliulilia

Neno "ule" linamaanisha mji wa Yerusalemu, lakini linawakilisha watu wanaoishi ndani ya mji huo.

Laiti ungelijua

Huu ni mshangao. Yesu alionyesha huzuni yake kwamba watu wa Yerusalemu hawakujua mambo haya. Maelezo haya yanaweza kuongezwa mwishoni mwa sentensi "hivyo mngeweza kuwa na amani." "Natamani mtambue au "nina huzuni kwa kuwa hamjui."

Wewe

Neno 'wewe' ni umoja kwa sababu Yesu alikuwa akizungumza na mji. Lakini kama hii haitakuwa na uhalisia katika lugha yako, unaweza kutumia wingi wa "wewe" kwa kutaja watu wa mji.

Yanmefichwa machoni pako

"Hamuawezi kuona tena" au "hamkuweza kufahamu"

Luke 19:43

Maelezo yanayounganisha

Yesu akaendelea kuongea.

Kwa

Kilichofuata ni sababu ya Yesu kuhuzunika.

Siku zinakuja juu yako

Hii inaonyesha kwamba wangepitia nyakati ngumu. Baadhi ya lugha hawaongelei juu ya wakati ujao. 'Katika siku zijazo mambo haya yatatokea kwako' au 'hivi karibuni utavumilia wakati mgumu.'

Wewe

neno 'wewe' ni umoja kwa sababu Yesu alikuwa akizungumza na mji. Lakini kama hii haitakuwa na uhalisia katika lugha yako, unaweza kutumia wingi wa "wewe" kwa kutaja watu wa mji.

Boma

Boma ni ukuta unaolinda watu wasitoke nje ya mji.

Watakuangusha chini kwenye ardhi

Kwa kuwa Yesu alikuwa akiongea na mji, hii inaelezea ukuta na wajenzi wa ukuta wa mji. "Wataharibu kuta zako" au "Wataharibu kuta zako."

Na watoto wako pamoja nawe

Hii inaelezea watu wanaoishi kwenye mji. "na watawaua watu wa kwenye mji."

Hawataacha jiwe moja juu ya lingine

Huu ni mfano unaoelezea namna ambavyo maadui wataharibu kabisa mji uliojengwa kwa mawe. "Hawataacha jiwe lolote kwenye eneo hilo."

Haukulitambua hilo

"haukulijua"

Luke 19:45

Maelezo yanayounganisha:

Hili ni tukio lingine kwenye sehemu hii ya simulizi. Yesu aliingia hekaluni.

Kufukuza

"Kutoa nje" au "kutoa kwa nguvu nje"

Imeandikwa

Hii imenukuliwa toka Isaya. "Maandiko yanasema" au "Nabii aliandika maneno haya kwenye maandiko"

Nyumba yangu

Neno "yangu" inamuelezea Mungu na "nyumba" linaelezea hekalu.

Nyumba ya sala

"sehemu ambayo watu wananiomba"

Pango la wanyang'anyi

"sehemu ambayo wanyang'anyi wanajificha." "Kama pango la wanyang'anyi."

Luke 19:47

Maelezo yanayounganisha.

Huu ni mwisho wa sehemu ya simulizi hii. Aya hizi zinaelezea kuhusu hatua inayoendelea baada ya sehemu kuu ya simulizi kuisha.

Hekaluni

'Hekaluni' au 'kwenye hekalu'

Makuhani wakuu

'Mwenye cheo cha juu cha makuhani' 'makuhani muhimu zaidi '

Walikuwa wakisikiliza kwa makini

"Walisikiliza kwa makini kile alichokuwa akikisema Yesu"

Luke 20

Luka 20 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri hupendelea kuweka mbele kidogo nukuu za Agano la Kale. ULB na tafsiri nyingine nyingi za Kiingereza huingiza mistari ya 20:17, 42-43, ambayo ni nukuu kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

Mtego

Sura hii ina maswali mawili yaliyopangwa ili kumkamata mtu anayekubali kitu ambacho hataki kusema. Yesu anauliza swali kwa Mafarisayo ambalo linawatega kwa kuwalazimisha kukiri kwamba wanaamini Yohana Mbatizaji alikuwa nabii au kuwakasirisha Wayahudi kwa kukataa hili. Viongozi walijaribu kumtega Yesu kwa kumuuliza kuhusu kulipa kodi kwa serikali ya Kirumi. Kujibu ndiyo kungewakasirisha Wayahudi na kujibu hapana kungewakasirisha Warumi. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#prophet)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Kitendawili

Kitendawili ni taarifa inayoonekana kuwa ya ajabu, ambayo ni kana kwamba inajikana yenyewe, lakini sivyo. Katika sura hii, Yesu ananukuu Zaburi ambayo inasema Daudi anamwita mwanawe "bwana," yaani, "mkuu." Hata hivyo, kwa Wayahudi, mababu walikuwa wakubwa kuliko uzao wao. Katika kifungu hiki, Yesu anajaribu kuwaongoza wasikilizaji wake kuelewa kweli kwamba Masihi mwenyewe atakuwa Mungu, na kwamba yeye mwenyewe ndiye Masihi. (Luka 20:41-44).

<< | >>

Luke 20:1

Maelezo yanayounganisha

Makuhani wakuu, mafarisayo na wazee walimuuliza Yesu hekaluni.

Ikawa

neno hili linaonyesha mwanzo wa sehemu mpya ya simulizi.

Luke 20:3

Taarifa ya jumla

Yesu anawajibu wakuu wa makuhani, mafarisayo na wazee.

aliwajibu na kuwaambia

"Yesu akawajibu"

Ilitoka mbinguni au kwa watu?

Yesu alijua mamlaka ya Yohana ilitoka mbinguni, Aliuliza swali ili vingozi wa kiyahudi waseme wanavyofikiri kwa wote waliowasikiliza. "mnafikiri mamlaka ya Yohana yalitoka mbinguni au kwa wanadamu?" au "mnadhani Mungu alimwambia Yohana abatize watu au watu walimwambia afanye hivyo?"

Toka mbingini

"toka kwa Mungu" Wayahudi waliepuka kumtaja Mungu kama "Yawe". Mara nyingi wanatumia neno "Mbingu" kumuelezea

Luke 20:5

Walijadiliana

"Walijadili" au "walitafakari jibu lao"

"tukisema imetoka mbinguni'

Lugha nyingine zinatumia nukuu ya moja kwa moja. "Kama tukisema mamlaka ya Yohana yalitoka Mbinguni"

Toka mbinguni

"Toka kwa Mungu" inategemea na namna ambavyo swali lilitafsiriwa kwenye mistari iliyopita, hii inaweza kutafsiriwa kama "Mungu alifanya" au "Mungu alimpa mamlaka"

Atasema

Yesu atasema

kutupia mawe

"Kutuua kwa kutupiga mawe" Sheria ya Mungu imeamuru watu wake kuwapiga mawe watu wanaomdhihaki yeye au manabii zake.

Luke 20:7

Ndipo wakamjibu

"ndipo wakuu wa makuhani na mafarisayo na wazee wakamjibu" Neno "ndipo" linaonyesha tukio limetokea kutokana na tukio limgine lililotokea kabla.

Walijibu kuwa hawakujua ilikotoka

Wakasema, "hatujui ilipotoka"

Imetoka wapi

"Yohana mbatizaji alitoka wapi." Mamlaka aliyokuwa nayo Yohana ya kubatiza yalitoka wapi" au "nani alimpa mamlaka Yohana ya kubatiza watu."

Nami sitawaambia

"Na sitawaambia" au "kama ambavyo hamniambii basi na mimi siwaambii"

Luke 20:9

Taarifa ya jumla

Yesu alaanza kuwaambia mfano watu waliokuwa hekaluni

Aliwakodisha wakulima wa mzabibu

"aliwaruhusu baadhi ya wakulima wa mizabibu watumie kwa mabadilishano ya pesa" au "aliwaruhusu wakulima wa mizabibu walitumie ba baadae wamlipe pesa"

Wakulima wa mizabibu

Watu ambao hupanda na kukuza mizabibu. "wakulima wa mizabibu"

matunda ya shambani

"Baadhi ya mizabibu" au "baadhi ya walichozalisha kwenye shamba." Pia inaweza kuelezea vitu amabavyo vinatokana na zabibu au pesa zinazotokana na mauzo ya zabibu

Wakamrudisha mikono mitupu

"wakamrudisha bila kumlipa" au "wakamrudisha bila mizabibu"

Luke 20:11

Wakamtendea vibaya

"Wakamdhalilisha"

Wakamjeruhi

"wakamsababishia majeraha"

Na wa tatu

Hata mtumishi wa tatu au na mtumishi mwingine. Neno

Luke 20:13

Wakati Wakulima wa mizabibu walipomuona

"wakati wakulima walipomuona mtoto wa mwenye shamba"

Tumuue

Walisema hivyo ili kutiana moyo kuua

Luke 20:15

Maelezo yanayounganisha

Yesu alimaliza kuwaambia mfano wake kwa makutano.

Walimtupa nje ya shamba

"Wakulima wa mzabibu walimtoa kwa nguvu mwana wa mwenye shamba nje ya shamba

Je bwana shamba atawafanya nini?

Yesu alitumia maswali ili wasikilizaji wake wawe makinijuu ya atakayoyafanya mwenye shamba. "sasa sikilizeni je Bwana shamba atawafanya nini."

Yasitokee haya

"Mungu ayaepushe yasitokee haya" au "Isitokee kamwe" Watu wanaelewa mfano huu kuwa unamaanisha kuwa Mungu atawaondoa Yerusalemu kwa kuwa wamemkataa Mesia. Wanaelezea kwa nguvu shauku yao kuwa jambo hili baya lisitokee.

Luke 20:17

Maelezo yanayounganisha

Yesu anaendelea kuwafundisha makutano

Yesu akawaangalia

"Lakini yesu akawatazama" au "Lakini Yesu akawaangalia moja kwa moja." Alifanya hivi ili wamuelewe alichokuwa anakisema.

Andiko hili lina maana gani?

"Andiko hili linaelezea nini?" Yesu alitumia maswali kuwauliza makutano. "Mnatakiwa kuwa na uwezo kuelewa aandiko hili"

Jiwe walilolikataa waashi limekuwa jiwe la msingi

Fumbo hili ni unabii toka kitabu cha Zaburi kuhusu namna watu watakavyomkataa Masiha.

Jiwe walilolikataa

"Jiwe walilolikataa waashi wakisema halikuwa zuri kwa ajili ya ujenzi." Kipindi hicho watu walijenga kuta za nyumba na majengo mengine kwa kutumia mawe.

Limekuwa jiwe la msingi

Hili lilikuwa jiawe la muhimu kwa kufanya jengo liwe imara. "Limekuwa jiwe la Msingi" au "limekuwa jiwe la Muhimu"

Kila atakayeanguka kwenye jiwe hilo.

"Yeyote atakayeanguka kwenye jiwe hilo". Fumbo hili ni unabii kuhusu kitakachotokea kwa wote watakaomkataa Mesia.

Atavunjika vipande vipande

"Atavunjika vipande vipande." Haya ni matokeo ya kuanguka kwenye jiwe.

Lakini kwa yeyote ambaye litamwangukia

"Lakini kwa yeyote ambaye jiwe litamwangukia." Fumbo hili linaonyesha unabii kuhusu Mesia atakapowahukumu waliomkataa.

Luke 20:19

Walitaka kumkamata

"walitafta njia ya kumkamata Yesu"

Wakati huo huo

Mda huo huo

Walikuwa wanawaogopa watu

Hii ndiyo sanbabu hawakumkamata Yesu moja kwa moja. Watu walimuheshimu Yesu na viongozi wa dini waliogopa kile ambacho watu wangekifanya ikiwa wangemkamata Yesu. "Lakini hawakumkamata kwa kuwa waliwaogopa watu."

Walituma wapelelezi

"Mafarisayo na Makuhani wakuu walituma wapelelezi kumuangalia Yesu"

Kama watapata kosa kwenye hotuba zake

"kwa kuwa walitaka kumtuhumu Yesu kwa kusema jambo baya"

ili kumpeleka

"ili kumpeleka kwa" au "ili kumkabidhi kwa"

Kwa uongozi na mamlaka ya Gavana

Kuongoza na mamlaka ni njia mbili za kuelezea kitu kimoja.

Luke 20:21

Maelezo yanayounganisha.

Hapa ni mwanzo wa tukio linalofuata kwenye sehemu ya simulizi hii. Muda sasa umepita tangu Yesu alipoulizwa maswali hekaluni na Makuhani wakuu. Wapelelezi sasa wanamuuliza Yesu.

Hawakushawishiwa na mtu yeyote.

Inamaanisha 1)wewe sema ukweli hata kama watu wa muhimu hwatapenda" au 2)"usimpendelee mtu mmoja juu ya mwingine."

Lakini fundisha ukweli kuhusu njia ya Mungu

Hii ni sehemu waliyosema wapelelezi kwamba wanafahamu kuhusu Yesu.

Je ni halali kwetu kulipa kodi kwa Kaisari.

Walitegemea kuwa Yesu atasema "ndio" au "hapana." Angesema "ndio" Wayahudi wangemkasirikia kwa kusema walipe kodi kwa serikali ya kigeni. Angesema "hapana" viongozi wa dini wangewaambia warumi kuwa Yesu aliawafundisha watu kuvunja sheria za warumi.

Ni halali

Walimuuliza Yesu kuhusu sheria za Mungu na sio sheria za Kaisari. "shheria zetu zinaruhusu."

Kaisari

kwa sababu kaisari alikuwa kiongozi wa serikali ya Roma hivyo wanaielezea serikali ya Roma kwa jina la Kaisari.

Luke 20:23

Yesu alielewa mtego wao

"lakini Yesu alitambua mtego wao ulivyokuwa" au " lakini Yesu alione kuwa walikuwa wanajaribu wanamtega" neno "wao" linamaanisha wapelelezi"

Dinari

Hii ni sarafu ya Kirumi yenye thamani ya mshahara wa siku.

Ni sura na chapa ya nani ipo juu yake

Yesu alitumia swali kuwajibu waliokuwa wanamtega.

Sura na chapa

"picha na jina"

Luke 20:25

Maelezo yanayounganisha

Hapa ni mwisho wa tukio hili kuhusu wapelelezi na sehemu ya simulizi inayoanza

Aliwaambia

"Kisha Yesu akawaambia"

Kaisari

Hapa "Kaisari" anamaanisha serikali ya Rumi

Hatukuweza kukosoa alichokisema

"hatukuweza kupata chochote kibaya kwa aliyoyasema"

Wakastaajabu

"Walishangaa" au wali

Luke 20:27

Taarifa ya jumla

Hii ni sehemu inayofuata ya simulizi. hatufahamu ilitokea wapi, japo inaweza kuwa wapo hekaluni. Yesu anaongea na Masadukayo.

Waliokuwa wanasema kuwa hamna ufufo

Maneno haya yanatambulisha Mawadukayo ambao ni kundi la Wayahudi wanaosema hakuna atakayefufuliwa toka kwa wafu. Haimaanishi kuwa baadhi ya masadukayo wanaamini kuwa kuna ufufuo na wengine hawaamini.

Ikiwa mtu akifiwa na kaka yake aliyekuwa na mke na hana mtoto.

"Ikiwa mtu akifiwa na kaka yake wakati ana mke lakini hawana watoto"

mtu atamchukua mke wa kaka yake

"mtu atamuoa mjane aliyefiwa na mume wake"

Luke 20:29

Maelezo yanayounganisha

Masadukayo wakamaliza kumuuliza Yesu maswali.

Taarifa ya jumla

Masadukayo walimwambia Yesu simulizi fupi kwenye mstari wa 29-32. Hii ni simulizi waliyoiweka kama mfano. kwenye mstari wa 33, walimuuliza Yesua swali kuhusu simulizi hiyo.

Walikuwepo ndugu saba

Hii inaweza kuwa imetokea au ni simulizi iliyotengenezwa ili kumjaribu Yesu.

Walikufa bila kuwa na watoto

"kufa bila kuwa na mtoto" au "na kufa lakini hawakuwa na mtoto yeyote"

Na wa pili pia

"wa pili alimuoa na kitu kilekile kikatokea" au "ndugu wa pili akamuoa na akafa bila kupata watoto"

Wa tatu akamchukua

"wa tatu akamuoa"

vivyo hivyo wa saba hakuacha watoto na akafa

"kwa njia ileile kama ndugu wote saba walimuoa na hawakupata watoto wa wakafa.

Kwenye ufufuo

"wakati watu watafufuliwa toka kwa wafu" au "wakati waliokufa wanakuwa hai tena." Baadhi ya lugha wananjia ya kuonyesha kuwa masadukayo hawaamini kuwa kuna ufufuo.

Luke 20:34

Maelezo yanayounganisha

Yesu anaanza kuwajibu Masadukayo

Wana wa ulimwengu huu

"Watu wa ulimwengu huu" au "watu wa nyakati hizi." Hii inapingana na wale walioko mbingini na watu watakaoishi baada ya ufufuo.

Kuoa na kuolewa

Kwa tamaduni hiyo wanaongelea juu ya mwanaume kumuoa mwanamke na mwanamke kupelekwa kwenye ndoa kwa mume wake "kuolewa."

Wao wanaostahili

"watu ambao Mungu anawaona kuwa wanastahili"

Kupokea ufufuo toka kwa waliokufa

"kufufuliwa toka kwa wafu" au "kufufuka toka kwa wafu"

Hawataoa wala hawataolewa

"Hawataoa." Hii ni baada ya ufufuo.

Hawatakufa tena

Hii ni baada ya ufufuo. "Hawatakuwa na uwezo wa kufa tena."

na wana wa Mungu watakuw wana wa ufufuo

"ni watoto wa Mungu maana amewatoa toka kwenye kifo"

Luke 20:37

Maelezo yanayounganisha.

Yesu alimaliza kuwajibu Masadukayo.

Lakini wafu wanafufuliwa, hata Musa alionyeshwa.

Neno "hata" lipo hapo kwa sababu Masadukayo hawakushangazwa na baadhi ya maandiko kuwa wafu wanafufuliwa, ila hawakutegemea kama Musa angeandika kitu kama hicho. "Lakini hata Musa alionyeshwa kuwa wafu wanafufuliwa"

Mahali panapohusu kichaka

"kwenye sehemu ya maandiko ameandika kuhusu kichaka kinachowaka moto" au "kwenye maandiko kuhusu kichaka kinachowaka moto"

Alipomuita Bwana

Ambapo Musa alimuita Bwana

Mungu wa Ibrahimu na Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo

"Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo" walimuabudu Mungu huyuhuyu.

Sasa

Neno hili limetumika kuonesha ukomo wa mafundisho makuu. hapa Yesu anaelezzea namna ambavyo simulizi hii inathibitisha kuwa watu wanafufuliwa.

Sio Mungu wa waliokufa bali wa waliohai

Sentensi hizi zina maana moja lakini ni mbili kwa ajili ya kusisitiza. Lugha nyingine zina namna tofauti ya kuonyesha msisitizo. " Bwana ni Mungu wa walio hai katika uzima wa milele"

Kwa sababu wote wanaishi kwake

"kwa sababu kwenye macho ya Mungu wote wapo hai." "kwa sababu Mungu anajua ruho zao zipo hai"

Luke 20:39

Baadhi ya mafarisayo wakajibu

"Baadhi ya mafarisayo wakamwambia Yesu." walikuwepo mafarisayo wakati Masadikayo walipokuwa wakimuuliza Yesu maswali.

Hawakuthubutu kumuuliza

"waliogopa kumuuliza" au hawakujitoa kumuuliza." hawakuendelea kumuuliza maswali ya mitego maana waliogopa majibu yake yenye hekima yatawafanya waonekane wajinga tena."

Luke 20:41

Taarifa ya jumla

Yesu aliwauliza Mafarisayo swali.

"Kwa nini wanasema.... mwanangu"?

Yesu alitumia swali kuwafanya mafarisayo wafikiri alichokuwa anakisema. "Tuwafikirie walivyosema... mwanangu" au "Nitaongea kuhusu wao wakisema... mwanangu"

Mwana wa Daudi.

"Kizazi cha Mfalme Daudi" Neno "mwana" limetumika kuelezea kizazi. Kwa sababu hii inamuelezea atakayetawala juu ya ufalme wa Mungu.

Bwana akasema kwa Bwana wangu

Hii imenukuliwa kutoka katika kitabu cha zaburi inasema "Yaweh" na mara nyingine inasema "Bwana" "Bwana Mungu akasema kwa Bwana wangu" au "Mungu akasema kwa Bwana wangu"

Bwana wangu

Daudi alikuwa akimuelezea Kristo kama "Bwana wake"

Mkono wangu wa kulia

upande wa kulia ni sehemu ya heshima. Mungu alimuheshimu Mesiya kwa kusema "keti upende wangu wa kulia"

Mpaka nitakapowaweka adui zako chini yako

Mpaka nitakapowashinda adui zako

Amekuwaje mwana wa Daudi?

"Imekuwaje Kristo akaawa mwana wa Daudi" "hii inaonyesha kuwa Kristo sio

Luke 20:45

Maelezo yanayounganisha

Sasa Yesu alikuwa anaelekeza umakini wake kwa wanafunzi wake na kuzungumza nao.

Jihadharini na

Kujihadhari navyo

Ambao hupenda kupita wamevaa mavazi marefu

Mavazi marefu yanaonyesha kuwa walikuwa wa muhimu. walipenda kupitapita wakiwa wamevaa nguo zao za muhimu"

Ambao Pia hula nyumba za wajane

"Pia wanakula kwenye nyumba za wajane" "Pia wanachukua kile kinachomilikiwa na wajane"

Wanajifanya wanasali sala ndefu

"wanajifanya kuwa ni wenye haki na huomba maombi marefu" au "huomba maombi maraefu ili watu wawaone"

Kujifanya

hii inamaanisha Mafarisayo walifanya mambo yaliyowafanya waonekane wana umuhimu na wenye haki kuliko walivyo kiuhalisia.

Hawa watapokea adhabu kubwa.

"Watapokea adhabu kubwa kuliko wengine" au "Mungu atawaadhibu zaidi ya wengine"

Luke 21

Luka 21 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Luka 21:5-36 ni mafundisho yaliyopanuliwa kuhusu kurudi kwa Kristo.

Dhana maalum katika sura hii

"Kwa maana wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, 'Mimi ndiye,'"

Yesu anafundisha kwamba kabla ya kurudi kwake watu wengi watajidai kuwa ni yeye anayerudi. Pia itakuwa wakati wa mateso makubwa.

"Mpaka nyakati za Mataifa zitimizwe"

Wayahudi walizungumzia wakati kati ya uhamisho wa Babeli na kuja kwa Masihi kama kipindi cha utawala wa Wayunani. Hii ni kwa sababu Wayahudi hawakuwa na mamlaka juu ya mambo yao wenyewe.

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Kusema kwa mifano

Unabii katika sura hii ina lugha ya kusema kwa mifano. Ni bora kutafsiri habari yalioandikwa kama matukio halisi isipokuwa tafsiri hii haiwezekani au inatoa maana isiyosawa. Kwa mfano, maneno "yamevunjwa," "yatasimama dhidi," na "hakuna nywele kichwani mwako itakayoangamia" ni mifano. "Ishara mbinguni," "tetemeko la ardhi," na "vita" lazima pia zitafsiriwe kwa uhalisi. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Mwana wa Binadamu"

Yesu anajiita mwenyewe kama "Mwana wa Binadamu." Lugha zingine haziwezi kuruhusu mtu kujitaja mwenyewe kama 'mtu wa tatu.'

<< | >>

Luke 21:1

mjane mmoja maskini

Hii ni namna ya kutambulisha mtu mpya katika hadithi

zawadi

"zawadi za fedha"

hazina

"sanduku la makusanyo" au "sanduku la fedha". Hili lilikuwa moja ya masanduku pale hekaluni ambapo watu huweka fedha kama zawadi kwa Mungu.

senti mbili

"sarafu mbili ndogo" au "sarafu za shaba ndogo sana". Hizi zilikuwa ni sarafu zenye thamani ndogo sana ambazo watu walizitumia siku hizo.

Nawaambieni

Yesu alikuwa akiongea na wanafunzi wake.

wametoa hizi zawadi kutoka katika vingi walivyonavyo

Tafsiri mbadala:"kuwa na fedha nyingi na kutoa baadhi ya hizo"

katika umaskini wake, ametoa zote

Tafsiri mbadala:"alikuwa na vichache sana, na bado aliweka vyote"

Luke 21:5

matoleo

"vitu ambavyo watu walimpa Mungu"

siku zitakuja ambazo

"kutakuwa na nyakati ambapo" au "siku fulani"

hakuna jiwe moja ambalo litaachwa juu ya jiwe jingine

"kila jiwe litatolewa mahali pake." Tafsiri mbadala: "adui hawataliacha jiwe juu ya jiwe juu ya jiwe jingine."

ambalo halitabomolewa

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. Tafsiri mbadala: "Yote yatabomolewa chini" au " Adui watabomoa chini kila jiwe."

Luke 21:7

wakamuuliza

"wanafunzi wakamuuliza Yesu" au "Wanafunzi wa Yesu wakamuuliza"

mambo haya

Hii inarejea kile ambacho Yesu amesema kuhusu adui kuliharibu hekalu.

kwamba msidanganywe

Yesu alikuwa akiwaambia wanafunzi wake.Tafsiri mbadala: "kwamba msiamini uongo" au "kwamba hakuna mmoja wa kuwadanganya."

kwa jina langu

Tafsiri mbadala: "wanadai kuwa mimi" au "wanadai kuwa na mamlaka yangu"

msiogope

"Msiruhusu haya mambo yawaogofye" au "msiogope"

mwisho hautatokea upesi

Tafsiri Mbadala: "mwisho wa dunia hautatokea upesi baada ya vita na vurugu" au "dunia haitafikia mwisho upesi baada ya mambo hayo kutokea"

mwisho

" mwisho wa kila kitu" au "mwisho wa miaka"

Luke 21:10

Kisha akawaambia

"Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake." Kwa sababu huu ni mwendelezo wa kuongea kwa Yesu kutokea kwenye mstari wa nyumba, baadhi ya lugha zisingependelea kusema "Kisha akawaambia."

Taifa litainuka kupigana na taifa jingine

Tafsiri mbadala: "taifa moja litashambulia taifa jingine"

Taifa

Hii inamaanisha makundi ya watu ya kikabila kuliko nchi.

Ufalme juu ya ufalme mwingine

Tafsiri mbadala: "Ufalme utainuka juu ya ufalme mwingine" au "majeshi kutoka ufalme mmoja utashambulia majeshi kutoka ufalme mwingine"

njaa na tauni

"kutakuwa na njaa na tauni" au "nyakati za njaa na magonjwa yanayouwa watu wengi"

matukio ya kutisha

"matukio yanayotisha watu" au "matukio yanayosababisha watu kuogopa sana"

Luke 21:12

mambo haya

Hii inamaanisha mambo mabaya ya kutisha ambayo Yesu alisema yatatukia.

wataweka mikono yao juu yenu

Tafsiri mbadala: "watawakamata" au "watawashika"

wata...

"watu wata.." au "adui wata..."

yenu

Yesu alikuwa akiongea na wanafunzi wake.

kuwapeleka kwenye masinagogi

"kuwatoa ninyi kwa viongozi wa masinagogi." Viongozi wa masinagogi wangewakataza Wayahudi wengine wote kuingiliana na wanafunzi kwa sababu wanamfuata Yesu.

na magereza

"na kuwapeleka ninyi magerezani" au "na kuwaweka ninyi magerezani"

kwa sababu ya jina langu

Tafsiri mbadala: "kwa sababu yangu" au "kwa sababu mnanifuata mimi"

kwa ushuhuda wenu

"kwa ninyi kuwaambia wao ushuhuda wenu kunihusu mimi"

Luke 21:14

Kwahiyo

"Kwa sababu ya hili." Yesu anatumia neno hili hapa kurejea kwenye kila kitu alichokisema.

amueni mioyoni mwenu

Tafsiri mbadala: "zingatieni akilini mwenu" au "amua kiuthabiti"

kutoandaa utetezi wenu

"kutokufikiri nini ambacho mtasema ili kujitetea kinyume cha mashitaka yao"

nitawapa maneno na hekima

"Nitawaambia maneno gani ya hekima ya kusema"

maneno na hekima

Tafsiri mbadala: "maneno ya hekima"

ambayo adui zenu wote hawataweza kuipinga au kuikataa kwamba ni uongo.

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. Tafsiri mbadala: "Adui zenu hawataweza kubishana na ninyi au kusema kwamba hamko sahihi" au "Adui zenu lazima wakubali kwamba mko sahihi."

Luke 21:16

mtatolewa pia na wazazi wenu, ndugu zenu, jamaa zenu na rafiki zenu.

Tafsiri mbadala: "wazazi wenu, ndugu zenu, jamaa zenu na rafiki zenu watawapeleka kwa wenye mamlaka"

watawaua baadhi yenu

"watawaua baadhi yenu." Pia inaweza kutafsiriwa kama 1) "wenye mamlaka watawaua baadhi yenu" au 2) "wale ambao watawaleta watawaua baadhi yenu." tafsiri ya kwanza ni kama iko sahihi zaidi.

kwa sababu ya jina langu

Tafsiri mbadala: "kwa sababu yangu" au "kwa sababu mnanifuata mimi"

lakini hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyenu utakaopotea.

Hii inaonyesha sehemu ndogo sana ya kiungo cha mwanadamu kusisitiza kwamba mtu katika ukamilifu wake hatapotea. Yesu aliishasema kwamba baadhi yao wanaweza kuuwawa. Kwahiyo baadhi walielewa kwamba hawatadhurika kiroho. Tafsiri mbadala: "Lakini mambo haya hayawezi kweli kuwadhuru ninyi" au "Hata kila unywele juu ya vichwa vyenu utakuwa salama.

katika kuvumilia kwenu

"kwa kusimama thabiti." Tafsiri mbadala: "Kama hamtaacha."

mtaziponya nafsi zenu

"mtapokea uzima" au "mtaishi milele"

Luke 21:20

Yerusalemu imezungukwa na majeshi

Tafsiri mbadala: "Majeshi yanauzunguka Yerusalemu"

kwamba uharibifu wake umekaribia

"kwamba itaharibiwa hivi karibuni" au "kwamba watauharibu muda si mrefu"

kimbia

"kimbia mbali kutoka kwenye hatari"

hizi ni siku za kisasi

"hizi ni siku za adhabu" au "huu ni wakati ambapo Mungu atauadhibu mji"

mambo yote yaliyoandikwa

Tafsiri mbadala: "mambo yote ambayo manabii wameandika katika maandiko matakatifu zamani za kale"

yatatimilika

Tafsiri mbadala: "yatatokea"

Luke 21:23

kutakuwa na adha kuu juu ya nchi

Yaweza kutafsiriwa kama 1) watu wakaao katika nchi watadhikika au 2) kutatokea maafa kabisa katika nchi.

ghadhabu kwa watu hawa

"kutakuwa na ghadhabu kwa watu hawa." Tafsiri mbadala: "hawa watu watapata uzoefu wa hasira ya Mungu" au "God atakasirika sana na atawaadhibu watu hawa."

wataanguka kwa ncha ya upanga

"watauwawa kwa ncha ya upanga." Tafsiri mbadala: "maaskari maadui watawauwa.

watachukuliwa mateka kwa mataifa yote

Tafsiri mbadala: "Maadui zao watawakama na kuwapeleka nchi nyingine"

Yerusalemu itakanyagwa na watu wa mataifa

Inaweza kutafsiriwa kama 1) watu wa Mataifa wataushinda Yerusalemu na kuukalia au 2) watu wa Mataifa watauharibu mji wa Yerusalemu au 3) watu wa Mataifa watawaharibu watu wa Yerusalemu.

wakati wa watu wa Mataifa umekamilika

Tafsiri mbadala: "wakati wa watu wa Mataifa umefika mwisho"

Luke 21:25

kutakuwa na dhiki ya mataifa

Tafsiri mbadala: "watu wa mataifa mbalimbali watadhikika" au "watu wa mataifa mbalimbali watakuwa na fadhaa nyingi"

katika hofu kutokana na mlio wa bahari na mawimbi

"kwa sababu watachanganywa na mlio wa bahari na mawimbi" au "sauti kubwa ya bahari na machafuko yake yatawatisha watu." Hii inaoneka kumaanisha dhoruba isiyokuwa ya kawaida au machafuko yanayotokea baharini.

mambo yatakayotokea juu ya dunia

"mambo ambayo yatatokea duniani" au "mambo yatakayotokea kwa dunia"

nguvu za mbingu zitatikiswa

Inaweza kutafsiriwa kama 1) vitu vya huko angani kama jua, mwezi, na nyota hazitaenda kwa utaratibu wake wa kawaida au 2) roho zenye nguvu sana huko mbinguni zitafadhaishwa. Tafsiri ya kwanza inapendekezwa. Tafsiri mbadala: "Mungu atatikisa vitu vyenye nguvu huko mbinguni.

Luke 21:27

Mwana wa Adamu

Yesu anarejea kwake mwenyewe

akija mawinguni

Tafsiri mbadala: "akija chini katika mawingu"

katika nguvu na utukufu mkuu

Hapa "nguvu" inawezekana inarejea katika mamlaka yake kuuhukumu ulimwengu. Hapa "utukufu" unaweza kurejea mwanga angavu. Mungu wakati mwingine anaonyesha ukuu wake na mwanga angavu sana. Tafsiri mbadala: "a nguvu na utukufu" au "atakuwa na wa nguvu na wa utukufu sana."

simameni

Wakati mwingine watu wanapoogopa, hujiinamisha chini ili kuepuka kuonekana au kuumizwa. Wakati wanapokuwa hawaogopi tena, wananyanyuka. Tafsiri mbadala: "simameni na ujasiri."

inueni vichwa vyenu

Tafsiri mbadala: "tazameni juu." Kwa kutazama juu, wataweza kumuona mwokozi akija kwao.

kwa sababu ukombozi wenu unasogea karibu

Tafsiri mbadala: "kwa sababu mkombozi wenu anakuja kwenu" au "kwa sababu Mungu mara atawaokoa"

Luke 21:29

Inapopukutisha majani yake

"Wakati majani yake yaanzapo kukuwa"

mnajionea wenyewe na kutambua

Tafsiri mbadala: "watu wanajionea wenyewe na kutambua"

kiangazi tayari kiko karibu

"kiangazi kiko karibu kuanza." Kiangazi katika Israel ni wakati wa ukavu sana, hivyo mazao huvunwa mwanzo wa kiangazi. Tafsiri mbadala: "wakati wa mavuno u tayari kuanza."

ufalme wa Mungu u karibu

Mungu atausimamisha ufalme wake hivi karibuni" Tafsiri mbadala: Mungu atatawala kama Mfalme hivi karibuni."

Luke 21:32

kizazi hiki

Inaweza kutafsiriwa kama 1) kizazi ambazho kitaona moja ya ishara ambazo Yesu aliziongelea au 2) kizazi amacho Yesu alikuwa anakizungumzia. Tafsiri ya kwanza ni kama iko sahihi zaidi.

hakitapita, mpaka

Tafsiri mbadala: "kitakuwa bado hai wakati..."

Mbingu na nchi zitapita

"Mbingu na nchi zitakoma kuwepo." Neno "mbingu" hapa linamaanisha anga na ulimwengu mwingine juu yake.

maneno yangu hayatapita

"maneno yangu hayatakoma kuishi" au "maneno yangu hayatashindwa kamwe." Tafsiri mbadala: "Nikisemacho hakika kitatokea."

Luke 21:34

ili kwamba mioyo yenu isije ikalemewa

Tafsiri mbadala: "ili msije mkawa mmetingwa na"

ufisadi

"tamaa isiyoweza kuzuiwa" au " kujiweka kwenye kutamani na kutumia vitu ambavyo vinakufanya ujisikie vizuri." Tafsiri mbadala: "Anasa nyingi."

mahangaiko ya maisha haya

"kujitaabisha au kujihangaisha sana kuhusu maisha haya"

kwa sababu siku ile itawajia ghafula

Wengine wangependa kuongeza habari elekezi: "Kwamba kama hamtakuwa waangalifu ile siku itawajia ghafula." Ujio wa siku hiyo utaonekana kuwa wa ghafula na wakutotarajiwa kwa wale ambao hawako na hawaisubiri.

ile siku

Tafsiri mbadala: "siku ambayo Mwana wa Adamu atakuja"

ghafula kama mtego

Tafsiri mbadala: "wakati ambapo hamuitarajii, kama mtego unapofunga ghafula kwa mnyama"

itakuwa juu ya kila mmoja

"itamuathiri kila mmoja" au "tukio la siku hiyo litamuathiri kila mmoja"

katika uso wa dunia nzima

Tafsiri mbadala: "katika eneo la dunia nzima" au "juu ya dunia nzima"

Luke 21:36

imara vya kutosha kuyaepuka haya yote

Inaweza kutafsiriwa kama 1) "imara vya kutosha kuyavumilia haya mambo" au 2) "kuweza kuyaepuka haya mambo."

haya yote yatakayotokea

"mambo haya yatakayotokea." Yesu alikuwa amewaambia si muda mrefu juu ya mambo mabaya ambayo yangetokea kama vile kuteswa, vita, na kuchukuliwa mateka.

kusimama mbele za Mwana wa Adamu

"Kusimama kwa ujasiri mbele ya Mwana wa Adamu." Hii inaweza kumaanisha wakati ambapo Mwana wa Adamu anamhukumu kila mmoja. Mtu ambaye hayuko tayari atamuogopa Mwana wa Adamu na hataweza kusimama kwa ujasiri.

Luke 21:37

wakati wa mchana alikuwa akifundisha

"wakati wa mchana angeweza kufundisha." Mistari inayofuata kuhusu vitu ambavyo Yesu na watu walifanya kila siku katika wiki kabla hajafa.

hekaluni

Tafsiri mbadala: "katika hekalu" au "kwenye uwanja wa ndani wa hekalu"

usiku alitoka nje

"usiku angeliweza kwenda nje ya mji" au "alikwenda nje kila usiku"

Watu wote

Tafsiri mbadala: "idadi ya watu wengi sana" au "karibu kila mmoja"

walimuijia asubuhi na mapema

"wangekuja asubuhi na mapema" au "walikuja mapema sana kila asubuhi"

kumsikiliza

"kumsikiliza akifundisha"

Luke 22

Luka 22 Maelezo ya Jumla

uundo na upangiliaji

Matukio ya sura hii hujulikana kama "jioni ya mwisho." Sikukuu ya Pasaka kwa njia nyingi inafanana na dhabihu ya Yesu kama kondoo wa Mungu.

Dhana maalum katika sura hii

Kula mwili na damu

Hadi leo, hatua hii inafanyika karibu na makanisa yote kukumbuka dhabihu ya Kristo kwa ajili ya dhambi za mwanadamu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

Agano Jipya

Yesu anataja Agano Jipya wakati wa jioni la mwisho. Agano Jipya ni chanzo cha utata kati ya wasomi. Kuna maoni mengi tofauti kuhusu wakati agano hili linapoanza na uhusiano wa kanisa na agano jipya. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#newcovenant)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Mwana wa Binadamu"

Yesu anajiita mwenyewe kama "Mwana wa Binadamu." Lugha zingine haziwezi kuruhusu mtu kujitaja mwenyewe kama 'mtu wa tatu.'

"hii ndiyo saa yako"

Katika tamaduni nyingi, kuna imani kwamba mambo mabaya hutokea tu katikati ya usiku, wakati watu wema wamelala. Maneno haya ni kejeli yanayoonyesha kwamba watu wanaomkamata Yesu wanatenda mabaya. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#evil)

<< | >>

Luke 22:1

Maelezo ya ujumla:

Hii ni sehemu inayofuata ya simulizi. Yuda anakubali kumsaliti Yesu. Mistari hii inatupa taarifa za msingi kuhusu sehemu hii ya simulizi.

Basi

Neno hili linatumika hapa sehemu mpya ya simulizi

sikukuu ya mkate usiyotiwa chachu

sikukuu hii ilikuwa inaitwa kwa jina hili kwa sababu wakati wa sikukuu, Wayahudi hawakula mkate ambao ulikuwa umetengenezwa na chachu. Tafsiri mbadala: "Sikukuu ambapo wangekula mkate usiyotiwa chachu"

Mkate usiyotiwa chachu

Huu ni mkate ambao hauna chachu au hamila ili kuufanya uumuke. Tafsiri mbadala: "Mkate bila Hamila."

ilikuwa imekaribia

"ilikuwa tayari sana kuanza"

namna ya kumuua Yesu

Makuhani na waandishi hawakuwa na mamlaka ya kumuua Yesu wao wenyewe, lakini walitegemea kupata watu wengine wa kumuua. Tafsiri mbadala: "Namna gani ambavyo wangesababisha Yesu kuuwawa" au "namna ambavyo wangesababisha mtu amuuwe Yesu."

waliwaogopa watu

Inaweza kutafsiriwa kama 1) "walikuwa na wasiwasi wa kile ambacho watu wangefanya" au 2) "walikuwa na wasiwasi kwamba watu wangemfanya Yesu mfalme."

Luke 22:3

Maelezo ya ujumla:

Huu ndio mwanzo wa matukio katika sehemu hii ya simuli.

Yesu akaingia ndani ya Yuda Iskariote

Hii inawezekana ilikuwa sawa na kupagawa na pepo.

wakuu wa makuhani

"viongozi wa makuhani"

wakuu

'viongozi wa walinzi wa hekalu'"

namna ambavyo atamkabidhi Yesu kwao

Tafsiri mbadala: "namna ambavyo angewasaidia kumkamata Yesu"

Luke 22:5

Wali..

"Wakuu wa makuhani na wakuu"

kumpa fedha

"kumpa Yuda fedha"

alilidhia

"alikubali"

alitafuta fursa ya kumkabidhi Yesu kwao mbali na kundi la watu

hiki ni kitendo kinachoendelea baada ya sehemu hii ya simulizi kuisha.

kumkabidhi

"kuwasaidia kumkamata Yesu"

mbali na kundi la watu

"kwa usiri" au "wakati ambapo hakuna kundi la watu wakimzunguka"

Luke 22:7

Maelezo ya ujumla:

Hii ni sehemu nyingine ya simulizi. Yesu anawatuma Petro na Yohana kuandaa kwa ajili ya chakula cha Pasaka. Mstari wa saba utatupa habari au taarifa za msingi kuhusu simulizi inavyoanza.

Siku ya mkate usiyotiwa chachu

"Siku ya mkate bila hamila" au "Siku ya chapati." Hii ilikuwa ni siku ambayo Wayahudi wangetoa nje ya nyumba zao mikate yote ambayo ilikuwa imetengenezwa na hamila. Kisha wangesherehekea sikukuu ya mkate usiyotiwa chachu au hamila kwa siku saba.

kondoo wa Pasaka lazima atolewe

Kila familia au kikundi cha watu wangemchinja kondoo na kumla pamoja, hivyo kondoo wengi sana walichinjwa. Tafsiri mbadala: "watu ilikuwa lazima wachinje kondoo kwa ajili ya chakula cha Pasaka."

ili tuje tukile

Yesu alikuwa anawajumuisha Petro na Yohana aliposema "tu.." Petro na Yohana wangekuwa sehemu ya kundi ambalo lingekula chakula kile.

mkatuandalie

Hili ni neno la kiujumla linalomaanisha "fanya tayari." Yesu si kwamba alikuwa akiwaambia Petro na Yohana kufanya mapishi yote.

unataka tufanyie hayo maandalizi

Neno "tu.." halimuhusishi Yesu. Yesu asingekuwa sehemu ya kundi ambalo lingeandaa chakula kile.

tufanye maandalizi

"kufanya maandalizi ya chakula" au "kuandaa chakula"

Luke 22:10

Akawajibu

"Yesu akawajibu Petro na Yohana"

mwanaume ambaye amebeba mtungi wa maji atakutana na ninyi.

"mtamuona mtu amebeba mtungi wa maji"

amebeba mtungi wa maji

"amebeba mtungi wenye maji ndani yake." Inawezekana angekuwa amebeba mtungi begani mwake.

Mfuateni kwenye nyumba ambayo ataingia

Tafsiri mbadala: "Mfuateni, na ingieni kwenye hiyo nyumba"

Mwalimu anakwambia

Hii inaanzisha nukuu elekezi ambapo Yesu aliwaambia wanafunzi wake nini cha kusema.

Mwalimu

Hii inaongela juu ya Yesu.

Kula Pasaka

"kula mlo wa Pasaka"

Luke 22:12

Atawaonyesha

"Mwenye nyumba atawaonyesha"

ghorofani

"vyumba vya juu ya nyumba"

Hivyo wakaenda

"Hivyo Petro na Yohana wakaenda"

Luke 22:14

Nina shauku kubwa

"Nimetaka sana"

Kwa maana nawaambieni

Hii sentensi inatumika kusisitiza umuhimu wa kile Yesu atakisema baada ya hicho.

mpaka itakapotimizwa

Inaweza kutafsiriwa kama 1) "mpaka kusudi la Sikukuu ya Pasaka litakapokuwa limetimizwa" au 2) "mpaka tutakapokula na kushangilia Sikukuu ya mwisho ya Pasaka." Tafsiri mbadala: "Mpaka Mungu atakapoitimiliza" au "mpaka Mungu atakapolitimiliza kusudi la Sikukuu ya Pasaka."

Luke 22:17

alipokwisha kushukuru

"alipokwisha toa shukurani kwa Mungu"

akasema

"akasema kwa mitume wake"

mgawane ninyi kwa ninyi

Tafsiri mbadala: "mgawane divai miongoni mwenu" au "ninyi wote mnywe divai kidogo kutoka katika hiki"

kwa maana nawaambia

Hii sentensi inatumika kusisitiza wa kile ambacho Yesu atakisema baada ya hiki.

mzao wa mzabibu

Hii inarejea "jwisi" ambayo inakamuliwa kutoka katika zabibu inayoota kwenye shamba la mizabibu. Divai inatokana na "jwisi" ya zabibu iliyochacha.

mpaka ufalme wa Mungu utakapokuja

Tafsiri mbadala: "Mpaka Mungu atakapoimarisha ufalme wake" au "mpaka Mungu atakapotawala katika ufalme wake.

Luke 22:19

mkate

Huu mkate ni ule ambao haukuwa na hamila ndani yake, hivyo ilikuwa na chapati.

akaumega

"akaukata" au "akauchana." Aliugawanya kwenye vipande vingi vingi au aliugawanya kwenye vipande viwili na akawapa mitume kugawana miongoni mwao.

Huu ni mwili wangu

Inaweza kutafsiriwa kama 1) "Huu mkate ni mwili wangu" au 2) "Huu mkate unawakilisha mwili wangu."

mwili wangu ambao umetolewa kwa ajili yenu

"mwili wangu ambao nitautoa kwa ajili yenu" au "mwili wangu ambao nitautoa sadaka kwa ajili yenu" Tafsiri mbadala: "mwili wangu, ambao nautoa kwa wenye mamlaka kuuuwa kwa ajili yenu."

Fanyeni hivi

"kula huu mkate"

kwa kunikumbuka mimi

"ili kunikumbuka mimi"

kikombe hiki

Neno "kikombe" linamaanisha au linarejea divai ndani ya kikombe. Tafsiri mbadala: "Divai kwenye kikombe hiki" au "Divai hii."

ni agano jipya katika damu yangu

"ni agano jipya, ambalo litatoa matunda kwa damu yangu" au "ni agano jipya ambalo litahalarishwa kwa damu yangu" au "linawakirisha agano jipya, ambalo Mungu ataliimarisha wakati damu yangu itakapomwagwa"

ambayo imemwagika kwa ajili yenu

"damu yangu, ambayo imemwagwa katika kifo kwa ajili yenu" au "damu yangu, ambayo itatoka katika vidonda vyangu kwa ajili yenu nitakapokufa." Yesu aliongea kuhusu kifo chake kwa kurejea mwili wake kuvunjwa na damu yake kumwagwa.

Luke 22:21

Yeye anisalitie

"Yeye atakaye nisaliti"

Kwa maana Mwana wa Adamu kwa kweli aenda zake

"Kwa kweli Mwana wa Adamu atakwenda" au "Kwa maana Mwana wa Adamu atakufa"

kama ilivyokwisha amuliwa

Tafsiri mbadala: "kama Mungu alivyokwisha amua" au "kama Mungu alivyokwisha kupanga"

Lakini ole kwa mtu yule ambaye kupitia yeye Mwana wa Adamu asalitiwa

Tafsiri mbadala: "Lakini ole kwa mtu yule amsalitie Mwana wa Adamu!" au "Lakini ni hatari kiasi gani kwa mtu yule amsalitie Mwana wa Adamu!"

Luke 22:24

Kisha yakatokea mabishano katikati yao

"Kisha mitume wakaanza kubishana wao kwa wao"

ni nani aliye mkubwa

Tafsiri mbadala: "watu wangefikiri ni wa muhimu sana"

Akawaambia

"Yesu akawaambia mitume"

wana ubwana juu yao

"wanatawala kwa ukatili juu yao" au "wanapenda kutumia nguvu juu yao"

wanaitwa

Watu inawezekana hawakuwafikiria wale watawala kama watawala wakuheshimiwa. Tafsiri mbadala: "walipenda kuitwa" au "walijiita wenyewe."

waheshimiwa watawala

Tafsiri mbadala: "wafadhili" au "viongozi wanaowasaidia watu"

Luke 22:26

haitakiwi kuwa hivi kwenu ninyi

"msifanye kama hivyo"

mdogo kabisa

Viongozi walikuwa mara nyingi watu wazima na waliitwa "wazee," "vijana wadogo" walikuwa na uwezekano mdogo wa kuongoza. Tafsiri mbadala: "enye umuhimu wa mwisho"

Kwa

Hii inaunganisha amri ya Yesu mstari wa 26 na mstari mzima wa 27. Inamaanisha kwamba mtu wa muhimu zaidi anatakiwa kutumika kwa sababu Yesu ni mtumishi.

yule anayetumika

"yule anayehudumia chakula" au "yule anayewahudumia waliokaa." Hii inamaanisha mtumishi.

yupi mkubwa....tumika?

"nani aliye wa muhimu....atumike?" Yesu anatumia swali kutambulisha jibu lake kwa swali la mitume kuhusu ukubwa. Tafsiri mbadala: "Nataka ninyi mfikiri kuhusu nani aliye mkubwa...atumike."

yule aketie mezani

"yule anayekula chakula"

si yule aketiye mezani?

Yesu anatumia swali jingine kuwafundisha wanafunzi. Tafsiri mbadala: "Bila shaka yule aketie mezani ni wa muhimu zaidi kuliko mtumishi!"

Na mimi bado ni kati yenu kama atumikaye

"Bado nawatumikia." Neno "bado" liko hapa kwasababu kunautofautishaji kati ya kile ambacho watu wangetegemea Yesu kuwa na kile ambacho kweli yuko.

Luke 22:28

mmeendelea kuwa nami katika majaribu yangu

"mmekaa nami katika mapito yangu"

Nawapa ninyi ufalme, kama vile Baba alivyonipa mimi ufalme

Lugha nyingine zinaweza hitaji kubadilisha mpangilio. "Kama baba alivyonipa mimi ufalme, nami nawapeni."

Nawapa ninyi ufalme

"Nawafanya ninyi watawala katika Ufalme wa Mungu" au "Nawapa ninyi mamlaka kutawala katika ufalme" au "Nitawafanya ninyi wafalme"

kama Baba alivyonipa mimi ufalme

"kama Baba alivyonipa mimi mamlaka kutawala kama mfalme katika ufalme wake"

Mtakaa kwenye viti vya enzi

Tafsiri mbadala: "mtafanya kazi kama wafalme" au "mtafanya kazi za wafalme"

Viti vya enzi

Tafsiri mbadala: "Viti vya wafalme" au "viti vilivyotengenezwa kwa wafalme"

Luke 22:31

Taarifa ya kijumla:

Yesu anaongea moja kwa moja na Simoni.

Simon, Simon

Yesu alilisema jina lake mara mbili kuonyesha kwamba kile ambacho alikuwa akiseme kwake kilikuwa cha muhimu sana.

awapate, ili awapepete

Neno "awa" linaonyesha mitume wote.

awapepete kama ngano

Hii inamaanisha kwamba Shetani alitaka kuwajaribu mitume ili kupata makosa.

Lakini nimekuombea

Hapa inamaanisha amemuombea kipekee kabisa SImoni.

kwamba imani yako isishindwe

"kwamba utaendelea kuwa na imani" au "utaendelea kunitegemea mimi"

Baada ya kuwa umerudi tena

"Baada ya kuanza kunifuata tena" au "Baada ya kuanza kunitumikia mimi tena"

ndugu zako

Hii inamaanisha wanafunzi wengine wa Yesu. Tafsiri mbadala: "Waamini wenzako" au "mitume wengine."

Luke 22:33

Jogoo hatawika leo, kabla hujanikana mara tatu kwamba unanijua

Mpangilio wa maneno unaweza kubadilishwa na kusomeka: "Utanikana mara tatu kwamba unanijua kabla jogoo hajawika siku hii ya leo"

Jogoo hatawika leo, kabla hujanikana

Hii inaweza kuongelewa kwa namna chanya: "Jogoo atawika siku hii ya leo mara tu baada ya kunikana."

Jogoo hatawika

Hapa, kuwika kwa Jogoo kunaonyesha muda fulani katika siku. Jogoo mara nyingi huwika kabla ya jua kuchomoza asubuhi.

siku hii

Siku ya Kiyahudi huanza wakati wa kuzama kwa jua. Yesu alikuwa anaongea baada ya jua kuwa limezama. Jogoo angeliwika muda mchache kabla ya asubuhi. Asubuhi ilikuwa sehemu ya "siku hii." Tafsiri mbadala: "Usiku wa leo" au "asubuhi."

Luke 22:35

Nilipowapeleka ninyi

Yesu alikuwa akiongelea kuhusu mitume wake.

mfuko

Mfuko ni begi la kuwekea fedha. Hapa inatumika kumaanisha "fedha."

kikapu cha vyakula

Tafsiri mbadala: "Begi la msafiri" au "chakula"

Je mlipungukiwa na kitu? Wakajibu, "Hapana."

Yesu anatumia swali kuwasaidia mitume kukumbuka namna ambavyo watu waliwahudumia vizuri walipokuwa wakisafiri. Tafsiri mbadala: Wakati ule...bado mlikuwa na kila kitu mlichokihitaji.' Na wanafunzi walikubali wakasema 'Ndiyo, tulikuwa na kila kitu tulichokihitaji."

Hakuna

"Hatukupungukiwa na kitu" au "Tulikuwa na kila kitu tulichokihitaji"

Yule ambaye hana upanga, imempasa auze joho lake.

Yesu alikuwa hamaanishi mtu falani kipekee ambaye hakuwa na upanga. Tafsiri mbadala:"Kama mtu hana upanga, anapaswa kuuza joho lake."

joho

"koti" au "nguo ya nje"

Luke 22:37

ambayo yameandikwa kwa ajili yangu

Tafsiri mbadala:"ambayo nabii ameandika kuhusu mimi katika maandiko"

lazima yatimilike

Mitume wangelimuelewa Mungu kwamba angesababisha yote yaliyoandikwa kwenye maandiko kutokea. Tafsiri mbadala: "Mungu atatimiliza" au "Mungu atayafanya yatokee."

alichukuliwa kama mtu ambaye anavunja torati

Hapa Yesu ananukuu maandiko. Tafsiri mbadala: " watu walimchukulia kama mtu ambaye hafuati au hana sheria."

Mvunja sheria

"Wale wanaovunja sheria" au "waharifu"

Kwa sababu kile kilichotabiriwa kwa ajili yangu

Inaweza kumaanisha 1) "Yale ambayo mtume ametabiri kuhusu mimi yako tayari kutokea" au 2) "Kwa kuwa maisha yangu yanafikia ukingoni."

wakasema

Hii inamaanisha angalau wawili wa mitume wa Yesu.

yatosha

Inaweza kumaanisha 1) "Hizo panga zinatosha" au 2) "Hiyo inatosha kuiongelea." Yesu aliposema wanatakiwa kununua panga, alikuwa hasa akiwaambia kuhusu hatari ambazo wote watazikabili. Inawezekana si kwamba aliwataka wanunue panga na wapigane.

Luke 22:39

Baada ya chakula cha usiku

Hii inamaanisha kukamilika kwa chakula cha Pasaka.

kwamba msiingie majaribuni

"kwamba hamjaribiwi" au "hakuna kitu cha kuwajaribu na kuwafanya kutenda dhambi"

Luke 22:41

mrusho wa jiwe

"kama umbali wa mtu kurusha jiwe." Tafsiri mbadala: "umbali mfupi" au kwa kipimo cha kukadilia kama "umbali wa mita 30"

Baba, kama unataka

Yesu atabeba adhabu ya dhambi zote katika historia ya mwanadamu kwa adhabu ya msalabani. Anaomba kwa Baba yake akimuuliza kama kuna njia nyingine.

Baba

Hiki ni cheo muhimu kwa Mungu

niondolee kikombe hiki

Yesu anamaanisha juu ya mateso ambayo yuko karibu kuyapitia kana kwamba yalikuwa ndani ya kikombe na kwamba alikuwa anakwenda kukinywa. Tafsiri mbadala: "niondolee hiki kikombe cha mateso" au "niondolee haya mateso" au "niokoe kutoka katika kuteseka kwa namna hii."

Lakini si kama nitakavyo mimi, lakini mapenzi yako yafanyike."

Tafsiri mbadala: "Hata hivyo, nataka kufanya yale ambayo ni sawasawa na mapenzi yako kuliko yale ambayo ni sawasawa na mapenzi yangu.

Luke 22:43

akamtokea

"akamtokea Yesu"

akamtia nguvu

"akamtia moyo"

Akiwa katika kuugua, akaomba

"Alikuwa katika kuugua, na akaomba"

Luke 22:45

Alipoamka kutoka katika maombi yake

Tafrisi mbadala: "Wakati Yesu alipoamka baada ya kuomba" au "Baada ya kuomba, Yesu aliamka na"

akawakuta wamelala kwa sababu ya huzuni nyingi

"aliwaona kwamba walikuwa wamelala kwa sababu walikuwa na huzuni sana"

Kwanini mnalala?

Inaweza kumaanisha 1) "Nashangazwa kwamba mnalala sasa" au 2) "Hampaswi kuwa mmelala sasa hivi!"

kwamba msiingie majaribuni

"msijaribiwe" au "hakuna kitu cha kuwajaribu na kuwafanya mtende dhambi"

Luke 22:47

tazama, kundi kubwa la watu likatokea

Neno "tazama" linatutazamisha kuhusu kundi jipya katika simulizi.

akiwaongoza

Yuda alikuwa akiwaonyesha watu Yesu alipo. Alikuwa hawaambii kundi la watu nini cha kufanya. Tafsiri mbadala: "akiwaongoza kwa Yesu."

ili ambusu

"kumsalimia kwa busu" au "kumsalimia kwa kumbusu." Wakati wanaume walipowasalimia wanaume wengine ambao walikuwa wa familia au marafiki, waliwakumbatia.

je unamsaliti Mwana wa Adamu kwa busu

Yesu anatumia swali kumkemea Yuda kwa kumsaliti kwa busu. Kwa kawaida busu ni ishara ya upendo. Tafsiri mbadala: "Ni busu unayotumia kumsaliti Mwana wa Adamu!"

Mwana wa Adamu

Yesu anatumia neno hili kujiongelea yeye.

Luke 22:49

wale waliokuwa karibu na Yesu

Hii inaonyesha wanafunzi wa Yesu.

hayo yanayotokea

Tafsiri mbadala: "kwamba makuhani na maaskari walikuwa na watu wa kumkamata Yesu"

akampiga mtumishi wa kuhani mkuu

"akampiga mtumishi wa kuhani mkuu kwa panga"

akagusa sikio lake

Tafsiri mbadala: "akamgusa mahali ambapo sikio lake lilikuwa limekatwa"

Luke 22:52

Je mnakuja kana kwamba mnakuja kupambana na mnyang'anyi, na marungu na mapanga?

"Je mnakuja na marungu na mapanga kwa sababu mnafikiri mimi ni mnyang'anyi?" Yesu anatumia hili swali kuwa tahayarisha viongozi wa Kiyahudi. Tafsiri mbadala: "Mnajua kwamba mimi si mnyang'anyi, na bado mnanijia mkileta mapanga na marungu."

Nilipokuwa pamoja nanyi siku zote

"Nilikuwa kati yenu kila siku"

hekalu

Tafsiri mbadala: "Uwanda wa ndani ya hekalu" au "katika hekalu"

kuweka mikono yenu juu yangu

Tafsiri mbadala: "kunikamata"

saa yako

"muda wako"

mamlaka ya giza

Hii inamaanisha mtawala muovu, Shetani. Tafsiri mbadala: "muda kwa mtawala wa giza" au "muda ambao Shetani anafanya mambo maovu kama anavyopenda kufanya"

Luke 22:54

wakamuongoza

"wakamuongoza Yesu kutoka kwenye bustani mahali ambapo walikuwa wamemkamata"

walikuwa wamewasha moto

Moto ulikuwa ni wakuwapa watu joto. Tafsiri mbadala: "baadhi ya watu walikuwa wamewasha moto."

katikati ya uwanda wa ndani

Huu ulikuwa uwanda katika nyumba ya kuhani mkuu. Ulikuwa na kuta pande zote, lakini bila paa.

Luke 22:56

akamtazama akamwambia

"akamtazama moja kwa moja Petro na kusema na watu wengine pale uwandani"

Huyu mtu pia alikuwa pamoja naye

Mwanamke alikuwa anawaambia watu kuhusu Petro kuwa na Yesu. Inawezekana kwamba hakulijua jina la Petro.

Lakini Petro akakana

"Lakini Petro akasema haikuwa kweli"

Mwanamke, mimi simjui

Petro hakulijua jina la yule mwanamke. Hivyo alikuwa hamtukani kwa kumuita "mwanamke".

Mwanaume, mimi siyo

Petro hakulijua jina la yule mwanaume. Hivyo alikuwa hamtukani kwa kumuita "mwanaume".

Luke 22:59

akasisitiza akasema

"alisema kwa msisitizo" au "alisema kwa sauti"

Kweli kabisa huyu mtu

Hapa "huyu mtu" inamaanisha Petro. Muongeaji inawezeka hakulijua jina Petro.

ni Mgalilaya

Mwanaume aliweza kuonyesha Petro alitokea Galilaya kutokana na jinsi alivyoongea.

sijui usemalo

Tafsiri mbadala: "kile ulichosema si kweli kabisa" au "kile ulichosema na uongo kabisa"

wakati akiongea

"wakati Petro alipokuwa akiongea"

Luke 22:61

neno la Bwana

Tafsiri mbadala: "Neno la Yesu" au "Kile ambacho Yesu alikuwa amekisema"

leo

Yesu alikuwa ameishaongea jioni iliyopita kile kitakacho tokea muda si mrefu kabla ya jua kuchomoza au katika kuchomoza kwa jua. Tafsiri mbadala: "Usiku wa leo."

Luke 22:63

Baada ya kumfunika macho

"Baada ya kuwa wamemfunika macho yake ili kwamba asiweze kuona"

Tabiri! Ni nani aliyekupiga?

Wale walinzi hawakuamini kwamba Yesu ni nabii. Badala yake waliamini kwamba nabii wa ukweli angemjua aliyempiga hata kama alikuwa hawezi kuona. Walimuita Yesu nabii, lakini walitaka kuonyesha kwamba hakuwa nabii. Tafsiri mbadala: "Jionyeshe kwamba wewe ni nabii. Tuambie nani amekupiga? au "Haloo nabii, nani amekupiga?"

Tabiri

"Kuongea neno kutoka kwa Mungu!" Taarifa kutokana na ukweli huu ni kwamba Mungu angelimwambia Yesu nani alimpiga kwa sababu Yesu alikuwa amefunikwa macho na hakuweza kuona.

Luke 22:66

Wakampeleka kwenye Baraza

Inaweza kumaanisha 1) "Wazee walimleta Yesu kwenye baraza" au 2) "Walinzi walimpeleka Yesu mbele ya baraza la wazee."

wakisema

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. Tafsiri mbadala: "Wazee wakamwambia Yesu"

tuambie

"tuambie kwamba wewe ni Kristo"

Kama nikiwaambia...Kama nikiwauliza

Yesu alisema kwamba haikuwa na maana kama angesema au angewauliza kusema, wasingejibu kwa ufasaha. Hizo sentensi mbili kwa pamoja zinaelezea mtazamo wa Yesu kwamba baraza lilikuwa kwa kweli halitafuti ukweli.

Kama nikiwaambia hamtaniamini

Hii ni moja ya maelezo ya kinadharia aliyoyatoa Yesu. Ilikuwa ni njia ya Yesu kujibu bila kuwapa sababu ya kusema kwamba alikuwa anahatia ya kukufuru.

kama nikiwauliza hamtanijibu

Haya yalikuwa maelezo ya pili ya kinadharia

Luke 22:69

kuanzia sasa

"kuanzia siku hii" au "kuanzia kutoka leo"

Mwana wa Adamu

Yesu alitumia sentensi hii kumaanisha Kristo. Alimaanisha kwamba alikuwa akijiongelea mwenyewe, lakini wazee iliwalazimu kuuliza kuona kama hivyo ndivyo kweli alikuwa akisema.

amekaa mkono wa kuume wa nguvu ya Mungu

Wayahudi walielewa kwamba hakuna hata mmoja ambaye angeweza kukaa pale.Waliiona hii ni sawa na kusema "atakuwa na Mungu kama Mungu."

nguvu ya Mungu

"Mungu mwenye nguvu zote." Hapa "nguvu" inamaanisha mamlaka yake kuu.

Kwa hiyo wewe ni Mwana wa Mungu?

Baraza lilimhukumu Yesu kusulubiwa kwa sababu alijithibitishia kwamba yeye alikuwa "Mwana wa Mungu," akijua Baraza litamhukumu kifo.

Mwana wa Mungu

Hiki ni cheo muhimu kwa Yesu.

Ninyi mmesema mimi ndiye

"Ndiyo, ni kama mlivyosema"

Kwanini bado tunahitaji tena ushahidi?

Walitumia swali kwa kuweka msisitizo. Tafsiri mbadala: "Hatuna haja tena ya kuwa na ushahidi!"

tumesikia kutoka katika kinywa chake mwenyewe

Tafsiri mbadala: "tumesikia moja kwa moja kutoka kwake kwamba anaamini yeye ni Mwana wa Mungu"

Luke 23

Luka 23 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

ULB huweka mbele kidogo mstari wa mwisho wa sura hii kwa sababu unaunganishwa zaidi na sura ya 24 kuliko sura ya 23.

Dhana maalum katika sura hii

"Walianza kumshtaki"

Watu hawa hawakuwa wakimshtaki Yesu kwa kufanya uovu, bali mashtaka yao yalikuwa ya uwongo. Waligeuza ukweli ili kumfanya Pilato kumhukumu Yesu kufa.

"Pazia la hekalu likagawanyika na kuwa vipande viwili"

Hii ni ishara muhimu. Pazia ilikuwa mfano ya utenganisho kati ya Mungu na mwanadamu. Mungu hakuweza kupatikana moja kwa moja kwa sababu ya utakatifu wake. Kifo cha Kristo kilibadilisha hii. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#holy)

Desturi ya Mazishi

Ilikuwa ni desturi katika Israeli ya kale kumzika mtu aliyeheshimika katika kaburi na kutumia mwamba mkubwa kuifunga.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Sioni kosa lolote katika mtu huyu.""

Baada ya swali moja rahisi, inaonekana kwamba Pilato anamtangaza Yesu kutokuwa na hatia haraka sana. Hii ni kwa sababu Luka hajaweka maelezo mengi ya mazungumzo ya Yesu na Pilato. Habari hii imeandikwa katika Injili nyingine.

<< | >>

Luke 23:1

Mkutano wote

"Viongozi wote wa Kiyahudi"

wakasimama

"kusimama" au "kusimama kwa miguu yao"

mbele ya Pilato

"kuwa mbele ya Pilato". Kusimama kwa kumuangalia Pilato"

akipotosha taifa letu

"kusababisha ghasia kwa kuelezea uongo kwa watu"

kwa kukataza tusitoe kodi

"kwa kuwaambia wasitoe kodi"

Luke 23:3

Pilato akamuuliza

"Pilato akamuuliza Yesu"

Wewe wasema

"Ulichokisema ni sawa" au " Ni kama ulivyo niuliza mimi"

makutano

"Mkusanyiko wa watu"

Sioni kosa kwa mtu huyu

"Sijaona kuwa mtu huyo ana hatia ya kitu chochote)

akiwachochea

"kusababisha ghasia miongoni"

kuanzia Galilaya na sasa yuko hapa

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. "Alianza kusababisha ghasia huko Galilaya na sasa anasababisha ghasia hapa"

Luke 23:6

aliposikia haya

"kusikia kuwa Yesu alianza kufundisha huko Galilaya"

kama

kama

mtu huyu

Hii inamaanisha Yesu

alipotambua

"Pilato akatambua"

alikuwa chini ya utawala wa Herode

Kifungu hiki hakitaji ukweli unaoelekea kuwa Herode alikuwa Mtawala wa Galilaya. "Yesu alikuwa chini ya utawala wa Herode kwasababu Herode alitawala Galilaya"

akatuma

"Pilato alituma"

ambaye mwenyewe

Hii inamaanisha Herode

kwa siku hizo

"Wakati wa sherehe za Pasaka"

Luke 23:8

alifurahi sana

"Herode alifurahi sana"

alitaka kumuona

"Herode alihitaji kumuona Yesu"

Alisikia habari zake

"Herode alisikia habari ya Yesu"

na alitamani

"Herode alitamani"

kuona baadhi ya miujiza anayoifanya

"kumuona yeye akifanya baadhi ya miujiza"

Herode alimhoji Yesu kwa maneno mengi

"Herode alimuuliza Yesu maswali mengi"

hakumjibu chochote

"Hakumjibu" au "hajampa Herode majibu"

walisimama

"walisimama pale"

kwa ukali kumshutumu

"walimshutumu Yesu kwa ukali" au "walimshutumu yeye kwa hasira"

Luke 23:11

na kumvika mavazi mazuri

Tafsiri hii haimaanishi walifanya hivyo ii kumuheshimu au kumjali Yesu. Walifanya hivyo kumdhalilisha na kumdhihak Yesui"

Herode na Pilato wakawa marafiki kuanzia siku hiyo

Maelezo yaha yana maanisha walianza urafiki kwasababu Herode alifurahia kitendo cha Pilato kumruhusu kumuhukumu Yesu. "Herode na Pilato wakawa marafiki kuanzia siku hiyo kwasababu Pilato alituma Yesu apelekwe kwa Herode ili akahukumiwe"

kabla

"kabla ya siku ile"

Luke 23:13

akawaita pomoja makuhani wakuu, watawala na umati wa watu

"Aliwaita Makuhani na watawala na umati wa watu kuja kukutana pamoja"

tazama nimemuhoji mbele yenu

"Nimemuuliza Yesu Mbele yenu". Nimemuhoji Yesu wakati ninyi mnashuhudia hapa"

na sikuona kosa

"Na sifikiri kwamba ana hatia"

Luke 23:15

Hapana, hata Herode hajaona

"Hata Herode hafikiri kwamba ana hatia" au "Hata Herode anafikiri kuwa hana hatia"

kwa

"kwasababu" au "tunjua hili ni kwasababu"

amemrudisha kwetu

"Herode alituma Yesu arudishwe kwetu" Neno "kwetu" linamaanisha Pilato na askari wake,na siyo makuhani na waandishi waliokwenda kwa Herode pamoja na Yesu, wala sio makutano.

hakuna chochote alichokifanya kinachostahili adhabu ya kifo

"hakufanya kitu chochote kinachostahili adhabu ya kifo"

Kwahiyo basi nitamuadhibu

Kwa sababu Pilato alikuwa hakuona kosa kwa Yesu anapaswa kumtoa bila adhabu. Siyo lazima kujaribu kufanya kauli hii iendane na tafsiri kifikra. Pilato alimuadhibu Yesu, ambaye alijua kuwa hana hatia, kwa sababu tu alikuwa na hofu ya umati wa watu.

Luke 23:18

wote wakapiga kelele pamoja

"Watu wote kwenye mkusanyiko walipiga kelele"

Mwondoe mtu huyu

"Mchukue mtu huyu mbali ". Mchukuwe mtu huyu mbali na kumnyonga"

ambaye amewekwa gerezani

"ambaye Warumi walimuweka gerezani"

kwa

"kwasababu ya kujihusisha" au " kwasababu ya uhalifu wake"

ya uasi fulani

"alijarubu kuwahamasisha watu wa mji kuasi dhidi ya serikali ya Kirumi"

Luke 23:20

akawaambia tena

"akaongea nao tena" au "aliongea tena na watu kwenye mkusanyiko"

akitamani kumuachilia Yesu

"kwasababu alitaka kumuachilia Yesu"

Akawaambia kwa maraya tatu

"Pilato akasema na mkutano tena, kwa mara ya tatu"

Luke 23:23

wakasisitiza

"Mkusanyo walisisitiza"

kwa sauti ya juu

"kwa kupiga kelele"

wakitaka asulubiwe

"Kwa Pilato kuwaamuru askari wake wamsulubishe Yesu"

Na sauti zao zikamshawishi Pilato

"Na umati wakandelea kupiga kelele hadi wakamshawishi Pilato"

kuwapa matakwa yao

"kufanya kile ambacho umati walitaka"

Akamuachilia yule waliyemtaka

"Pilato akamuachilia Barnaba ambaye umati walimuomba aachiliwe"

Aliyefungwa Jela

"ambaye Warumi walimuweka Jela"

Akamtoa Yesu kwa matakwa yao

"Pilato aliwaruhusu umati wafanye kwa Yesu chochote walivyotaka" au "Pilato alimtoa Yesu kwa umati wa watu na kuwaruhu umati kufanya kwa Yesu kile walicho kitaka."

Luke 23:26

Walipokuwa wakimpeleka

"wakati maaskari wakimpeleka Yesu mbali na alipokuwapo Pilato"

walimkamata Simon wa Ukirene

Maaskari wa Kirumi wana mamlaka ya kuwashurutisha watu kuwabebea mizigo yao". Usitafsiri kana kwamba Simoni amekamatwa au alifanya kosa fulani.

mmoja

"mtu aitwaye "

akitokea katika nchi

"aliyekuwa anakuja Yerusalemu akitokea nje ya mji"

wakamtwika msalaba

"kuweka msalaba juu ya mabega yake"

Luke 23:27

waliomboleza kwa ajili yake

"kuomboleza kwa ajili ya Yesu"

wakimfuata

"waliokuwa wakimfuata Yesu"

Mabinti wa Yerusalemu

"Mabinti" wa mji maana yake watu wa mji . "ninyi wanawake mliotoka Yerusalemu"

msinililie mimi

"kulia kwaajili ya hali yangu"

bali jililieni ninyi wenyewe na kwa ajili ya watoto weno

"badala yake mlie kwa ajili ya mambo yanayokwenda kutokea kwa ajili yenu na watoto wenu"

Luke 23:29

ambao watasema

"watu watakaposema"

waliotasa

"wanawake ambao hawakuzaa watoto"

ndipo

"Kwa wakati huo"

kuambia milima

"wataiambia milima"

Maana kama wakifanya mambo haya ikiwa mti mbichi, itakuwaje kwa mti uliokauka?

Yesu anatumia swali kusaidia umati kuelewa kwamba watu wanafanya mambo mabaya sasa katika nyakati nzuri, hivyo kwa hakika watafanya mambo mabaya zaidi katika nyakati mbaya siku zijazo. "Unaweza kuona kwamba wanafanya mambo hayo mabaya wakati mti ni mbichi, hivyo unaweza kuwa na uhakika kwamba watafanya mambo kuwa mabaya wakati mti ni kavu."

mti mbichi (kijani)

mti mbichi(kijani) ni mfano wa kitu kilichokizuri kwa sasa . Kama lugha yako ina mfano mzuri unaweza kutumia hapa.

uliokauka

"Mti uliokauka ni mfano wa kitu kibaya baadaye"

wakifanya

hapa alikuwa akimaanisha aidha Warumi au viongozi wa kiyahudi au hakuna aliyelengwa moja kwa moja "

Luke 23:32

wanaume wengine, wahalifu wawili, walipelekwa pamoja naye ili wauwawe

"Maaskari waliwapeleka wahalifu wengine wawili pamoja na Yesu ili wakauwawe pia.

Luke 23:33

walipofika

Neno "walipofika" inajumuisha maaskari, wahalifu na Yesu.

wakamsulunisha

"maaskari wakamsulubisha Yesu"

mmoja upande wa kulia

"mmoja wa wahalifu aliwekwa upande wa kulia wa Yesu"

na mwingine upande wa kushoto

" na muhalifu mwingine aliwekwa upande wa kushoto mwa Yesu"

Baba, uwasamehe wao

Neno "wao" inamaanisha wale wanao msulubisha Yesu. Yesu aliongea kwa huruma na Baba yake juu ya wanaume waliokuwa wanamsulubisha"

Baba

Hii ni cheo muhimu kwa Mungu

kwa kuwa hawajui watendalo

"kwasababu hawajui kile wanachokifanya". Maaskari hawakujua kuwa wanamsulubisha Mwana wa Mungu. Kwasababu hakika hawamjui ni nani wanayemsulubisha"

wakapiga kura

Maaskari walifanya aina ya kamari "walifanya kamari"

kugawa mavazi yake

"kuamua nani kati ya maaskari atapeleka nyumbani sehemu ya mavazi ya Yesu"

Luke 23:35

walisimama

"walisimama pale"

Yeyey

Hii inamaanisa Yesu.

ajiokoe mwenyewe

"Yesu atakuwa na uwezo wa kujiokoa" au "Tunataka kuona akijionyesha yeye ni nani kwa kujiokoa mwenyewe kutoka msalabani"

aliyechaguliwa

"mmoja ambaye Mungu alimchagua"

Luke 23:36

yeye

"Yesu"

walimkaribia yeye

"kuja karibu na Yesu"

wakampa siki

" walimpa Yesu siki ili anywe" Siki ni aina ya kinyaji kirahisi ambayo watu wa kawaida hunywa. Maaskari walimdhihaki Yesu kwa kumpa siki mtu aliyesema yeye ni mfalme.

alama juu yake

" kitu kama ubao juu ya msalaba wa Yesu iliyoandikwa"

HUYU NDIYE MFALME WA WAYAHUDI

Watu walioweka alama juu ya Yesu walikuwa wakimdhihaki yeye. Hawakuamini kweli kuwa yeye ni mfalme.

Luke 23:39

Aliyesulubiwa

"aliyeangikwa pia msalabani"

alimtukana

"alimtukana Yesu"

Wewe si Kristo?

Muhalifu alitumia swali kumdhihaki Yesu."umedsi kuwa wewe ni Kristo"

Jiokoe mwenyewe na sisi pia

Muhalifu hakufikiri kweli kuwa Yesu angeweza kuwaokoa kutoka kwenye msalaba"

yule mwingine akajibu

"muhalifu mwingine alijibu"

akimkemea na kusema

"na kumkemea yule muhalifu akisema"

Je wewe humuogopi Mungu, kwani uko katika hukumu hiyo hiyo

Muhalifu alitumia swali kumkemea yule muhalifu mwingine. " Hauna hofu ya Mungu , kwani unamdhihaki Yesu wakati umetundikwa msalabani kama yeye.

sisi tupo hapa kwa haki

"Kiukweli sisi tunastahili adhabu hii"

mtu huyu

Hii inamaanisha Yesu.

Luke 23:42

Na akaongeza

"Muhalifu pia akasema "

utakapokuja katika ufalme wako

"Utakapo anza kutawa kama Mfalme"

Ukweli nakuambia

"Ukweli" inaongeza msisitizo wa kile ambacho Yesu anaongea. "Nataka wewe uelewe kuwa"

Paradiso

Hii ni sehemu ambayo watu wema huenda wanapokufa. Yesu alikuwa akimthibitishia mtu yule kuwa atakuwa na Mungu na Mungu atamkubali yeye. "Ni mahali pa furaha" au 'Ni mahali pa watu wenye haki" au "Ni mahali ambapo watu wanaishi vizuri."

Luke 23:44

ilikuwa karibu saa sita

"Ilipokaribi mchana" . Hii huonyesha desturi ambayo watu huanza kuhesabu saa kuanzia saa 12 asubuhi.

giza likaja juu ya ardhi yote

"ardhi yote ikawa giza"

hadi saa tisa

"Hadi 9 Mchana" Hii huonyesha desturi ambayo watu huanza kuhesabu saa kuanzia saa 12 asubuhi.

pazia la hekalu

"Pazia ndani ya Hekalu"

likagawanyika katikati

"ilichanika vipande viwili" . "Mungu alichana pazia la hekalu katika vipande viwili"

Luke 23:46

Akilia kwa sauti kuu, Yesu alisema, "Baba mikononi mwako naiweka roho yangu,"

Mungu Baba alikuwa amemtuma Mungu Mwana kufa msalaba ili afanyike sadaka ya mwisho kwa ajili ya dhambi za binadamu. Lakini, Mwana bado alimpenda Baba na kumkabidhi maisha yake kwa Baba yake

Akilia

"kupasa sauti"

Baba

Hii ni cheo muhimu kwa Mungu

mikononi mwako naiweka roho yangu

"Naiweka roho yangu kwako" au " Nakupa roho yangu, nikijua utaitunza"

baada ya kusema hivyo

"Baada ya Yesu kusema hivyo"

akafa

"Yesu akafa"

yaliyotendeka

"mambo yaliyotokea"

Luke 23:48

umati

"Mkusanyiko wa watu"

tukio

"tukio"au "kile kinachotokea"

waliokuja pamoja

"waliokusanyika pamoja"

mambo yaliyofanyika

"kitu kilichofanyika"

walirudi

"kurudi majumbani mwao"

wakipiga matiti yao

"wakipiga vifuani mwao wakionyesha jinsi walivyosikitika"

marafiki zake

"wale waliomjua Yesu" au "wale waliokutana na Yesu huko nyuma"

waliomfuata yeye

"walimfuata Yesu"

kwa mbali

"umbali fulani kutoka alipo Yesu"

hayo mambo

"yaliyotokea"

Luke 23:50

Tazama, palikuwa na mtu

Neno 'tazama' inatufanya tuweze kumuona mtu mpya katika hadithi. Lugha yako inaweza kuwa njia ya kufanya hili. "Kulikuwa na mtu ambaye alikuwa".

ambaye ni mmoja wa baraza

"na Yeye alikuwa mmoja wapo wa wajumbe wa baraza la Wayahudi"

mzuri na mwenye haki

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. "Yeye alikuwa mtu mzuri na mweye haki"

alikuwa hajakubaliana na maamuzi au matendo yao

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya." Joseph hakukubaliana na uamuzi wa baraza hilo kumuua Yesu na hatua ya baraza hilo"

kutoka Armathaya, Mji wa Kiyahudi

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya." Josefu alitokea kwenye mji wa kiyahudi ulioitwa Arimathaya"

ambaye alikua akisubiri

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya."Josefu alikuwa akisubiri"

Luke 23:52

Mtu huyu

"Josefu "

alimkaribia Pilato, akaomba

"alikwenda kwa Pilato na kuomba"

Alimshusha chini

"Josefu alichukua mwili wa Yesu kutoka msalabani"

akauzungushia sanda

"Akafunga mwili katika nguo nzuri ya kitani'

akamweka katika kaburi

"kuweka mwili wa Yesu kwenye kaburi" au "Kuweka mwili wa Yesu kwenye chumba cha kuzikia"

lililokuwa limechongwa katika jiwe

"Kaburi ambalo mtu alilichonga kwenye mwamba"

ambalo hakuna aliyewahi kulazwa

Hii inaweza ikatafsiriwa kama sentensi mpya. "Hakuna aliyewahi kuweka mwili katika kaburi hilo"

Luke 23:54

Ni siku ya maandalizi

"Ni siku ambayo watu wanajiandaa kwa siku ya Wayahudi kupumzika iitwayo Sabato"

Sabato inakaribia

"Inakaribia kuwa jioni, kuanza kwa Sabato" Alfajiri hapa ni mfano kwa ajili ya mwanzo wa siku. Kwa Wayahudi, siku ilianza jioni.

waliokuja nao kutoka Galilaya

"waliosafiri na Yesu kutoka jimbo la Galilaya"

walimfuata baada

"walimfuata Josefu na wanaume waliokuwa pamoja naye"

wakaona kaburi

"wanawake wakaona kaburi"

na jinsi mwili wake ulivyolazwa

"Wanawake waliona jinsi hao wanaume walivyomlaza mwili wa Yesu ndani ya kaburi"

walirudi

"wanawake walienda kwenye nyumba ambayo wanawake hao wanakaa"

kuandaa manukato na marashi

"kuandaa manukato na marashi ili kuandaa Mwili wa Yesu kwa ajili ya mazishi".

walipumzika

"wanawake wale hawakufanya kazi"

kulingana na amri

"Kulingana na sheria za Wayahudi" au "kama sheria ya Wayahudi inavyotaka"

Luke 24

Luka 24 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Imani ya wanawake

Katika sura hii inaonekana kuwa Luka kwa makusudi anatofautisha imani ya wanawake na imani ya wanafunzi kumi na wawili.

Ufufuo

Luka katika sura hii anatumia maelezo mengi ili kuonyesha ufufuo wa Yesu kutoka kwa wafu. Luka anaonyesha kwamba haikuwezekana kwa mtu mwingine kufa kwa niaba ya Yesu. Anaonyesha pia kwamba ufufuo haukuwa mfano. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#resurrection and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Mwana wa Binadamu"

Yesu anajiita mwenyewe kama "Mwana wa Binadamu." Lugha zingine haziwezi kuruhusu mtu kujitaja mwenyewe kama 'mtu wa tatu.'

"Siku ya tatu"

Inasemekana kuwa Yesu alifufuka kutoka wafu siku ya tatu. Alikufa siku ya Ijumaa alasiri (kabla ya kutua kwa jua) na kufufuliwa Jumapili. Katika Israeli ya kale, siku ilianza na kumalizika wakati wa kutua kwa jua. Pia walihesabu sehemu yoyote ya siku kama "siku."

Watu wawili wenye mavazi ya kuangaza

Mathayo, Marko, Luka, na Yohana wote waliandika juu ya malaika waliovalia nguo nyeupe wakiwa pamoja na wanawake katika kaburi la Yesu. Waandishi wawili kati yao waliwaita wanaume, lakini ni kwa sababu tu malaika walikuwa katika hali ya kibinadamu. Waandishi wawili waliandika kuhusu malaika wawili, lakini waandishi wengine wawili waliandika juu ya moja tu. Ni bora kutafsiri kila moja ya vifungu hivi kama inavyoonekana katika ULB bila kujaribu kufanya vifungu vyote kufanana. (Angalia: Mathayo 28:1-2, Marko 16: 5 na Luka 24: 4 na Yohana 20:12)

__<< | __

Luke 24:1

Mapema sana siku ya kwanza ya wiki

"Kabla jua halijachomoza siku ya Jumapili"

walikuja

"wanawake walifika kwenye."

kaburini

Kaburi lilikuwa limechongwa katika mwamba wa karibu na bahari.

jiwe limeviringishwa

Tafsiri mbadala: "kwamba mtu fulani alikuwa ameriviringisha lile jiwe"

jiwe

Hili lilikuwa kubwa, limechongwa, jiwe la duara kubwa la kutosha kuweza kuziba kabisa mlango wa kuingilia kaburini. Lilihitaji watu wengi kulivingirisha.

Luke 24:4

Ilitokea

Hii sentensi ilitumika hapa kuweka alama ya tukio muhimu katika simulizi.

mavazi ya kung'aa

"wamevaa angavu, mavazi yanayong'aa"

wamejaa hofu

"wakaogopa"

Kwanini mnamtafuta aliye hai miongoni mwa wafu?

Wale wanaume wanatumia swali kuwapinga wale wanawake kumtafuta kwenye kaburi mtu aliyehai. Tafsiri mbadala: " Mnamtafuta mtu aliye hai kati ya au miongoni mwao wafu" au "Hamtakiwi kumtafuta mtu ambaye yu hai katika sehemu wanapozika watu waliokufa!"

Kwanini mnamtafuta

Hapa inamaanisha wengi, inaongelea juu ya wanawake waliokuja.

Luke 24:6

Kumbukeni alivyo..

"Kumbukeni yale"

alivyosema nanyi

Yesu alikuwa amekwisha kusema haya wiki moja mapema.

nanyi

Neno "nanyi" linaonesha wingi. Inaongelea juu ya wale wanawake na wanafunzi wengine.

kwamba Mwana wa Adamu

Huu ni mwanzo wa kunukuu jambo si kwa njia ambayo imenyooka.

Mwana wa Adamu lazima atolewe kwenye mikono ya watu wenye dhambi na asulubishwe.

Hii ni jamboa bila shaka lingetokea kwa sababu alikuwa ameamua kwamba litatokea. Tafsiri mbadala: "ilikuwa ni lazima wamtoe Mwana wa Adamu kwa watu wenye dhambi ili waweze kumsulubisha .

kwenye mikono

Hapa "mkono" unaonyesha nguvu au uthibiti.

Luke 24:8

wakakumbuka maneno yake

Tafsiri mbadala: "walikumbuka yale aliyoyasema Yesu"

wengine wote

"wanafunzi wengine wote waliokuwa na mitume kumi na mmoja"

Basi

Neno hili limetumika hapa kuonyesha pumziko katika simulizi kuu. Hapa Luka anatoa majina ya baadhi ya wanawake na kuelezea namna ambavyo mitume waliitikia kwa kile ambacho walisema.

Luke 24:11

Lakini ujumbe huu ukaonekana kama mzaa tu kwa mitume

"Lakini mitume walifikiri kwamba kile ambacho wanawake walisema yalikuwa ni maongezi yasiyo na maana"

akichungulia na kuangalia ndani

"akainama." Petro ilimlazimu ainame ili aweze kuangalia au kutazama kaburini.

sanda ziko peke yake

"sanda tu"

Luke 24:13

Tazama

Hii inaashiria mwanzo wa tukio jingine tofauti na lile linalowahusisha wale wanawake na Petro.

siku hiyo hiyo

"siku ile ile "

Emmau

Hili ni jina la mji

maili sitini

"kilometa kumi na moja."

Luke 24:15

Ikatokea kwamba

Hii sentensi inatumika hapa kuashiria pale ambapo kitendo kinaanza. Kinaanza na Yesu kuwasogelea karibu.

macho yao yalizuiliwa katika kumtambua yeye

Tafsiri mbadala: "Kuna kitu kiliwazuia hivyo hawakuweza kumtambua."

Luke 24:17

Cleopa

Hii ni jina la mwanamume

Je wewe ni mtu pekee ...siku hizi?

Cleopa anatumia swali kuonyesha mshangao wake kwamba huyu mtu anaonekana kutokujua juu ya mambo ambayo yametokea Yerusalemu.

Luke 24:19

Mambo gani?

"Mambo gani yametokea?" au "Mambo gani yaliyofanyika?"

muweza katika matendo na maneno mbele za Mungu na watu wote

Hii inamaanisha kwamba Mungu alimfanya Yesu kuwa mwenye nguvu na kwamba watu walimuona kwamba alikuwa muwez. Tafsiri mbadala: "na Mungu alimpa nguvu kufanya na kufundisha mambo makubwa ambayo yaliwashangaza watu wote."

walivyomtoa kuhukumiwa kifo na kumsulubisha

Tafsiri mbadala: "walimtoa Yesu kwa kiongozi wa Kirumi ili kiongozi huyo aweze kumuua kwa kumsulubisha"

Luke 24:21

atakaye waweka huru Israel

Warumi walitawala juu ya Wayahudi. Tafsiri mbadala: "atakaye tuweka huru Waisraeli kutoka kwa adui zetu wa Kirumi."

tangu mambo haya yatokee

"tangu walipomuua"

Luke 24:22

Lakini pia

Wale wanaume waliichukulia taarifa ya wale wanawake kuwa ni kitu kizuri, siyo kitu kingine kibaya cha kuongezea juu ya kifo cha Yesu.

baada ya kuwapo kaburini

Wale wanawake ndiyo waliokuwa pale kaburini.

maono ya malaika

"malaika katika maono"

Luke 24:25

mioyo mizito ya kuamini

Tafsiri mbadala: "akili zenu ni nzito sana kuamini" au "ninyi ni wazito kuamini"

Je haikuwa lazima ...utukufu?

Yesu anatumia swali kuwakumbusha wanafunzi juu ya kile ambacho manabii walisema. Tafsiri mbadala: "Ilikuwa ni lazima...utukufu."

kuingia katika utukufu wake

Hii inamaanisha juu ya nyakati ambazo Yesu atamuonyesha kila mmoja uzuri wake na ukuu wake na kupokea heshima na ibada.

Luke 24:28

Walipokaribia

"Walipokuja karibu"

Yesu alifanya kana kwamba anaendelea mbele

Wale watu wawili walieelewa kutokana na kitendo chake kwamba alikuwa anaendelea kuelekea sehemu nyingine. Inawezekana labda aliendelea kutembea barabarani walipochipuka kuingia kwenye geti la kijiji. Hakuna kiashiria kwamba Yesu aliwadanganya kwa maneno.

Wakamsihi

"Walimuomba kwa nguvu sana." Neno la kiyunani linamaanisha kutumia nguvu za mwili juu ya muda wa ziada. Iliwachukua muda fulani na jitihada fulani kumshawishi.

Yesu akaingia

"Yesu akaingia ndani ya nyumba"

Luke 24:30

Ilitokea

Neno hili limetumika hapa kuashiria tukio muhimu katika simulizi.

mkate

Hii inazungumzia juu ya mkate unaotengenezwa bila hamila. Haimaanishi chakula kwa ujumla.

akaubariki

"akashukuru kwa ajili ya huo mkate" au "Akamshukuru Mungu kwa ajili ya mkate"

Kisha macho yao yakafunguliwa

Tafsiri mbadala: "kisha wakaelewa" au "kisha wakatambua"

akatoweka ghafla mbele ya macho yao

Hii inamaanisha kwamba ghafula hakuwa tena pale. Haimaanishi kwamba akawa haonekani kwa macho.

Hivi mioyo yetu haikuwaka... maandiko?

Wanatumia swali kuweka msisitizo namna walivyo shangazwa juu ya kukutana kwao na Yesu. Tafsiri mbadala: "Mioyo yetu ilikuwa ikiwaka ndani yetu...maandiko."

ikiwaka ndani yetu

Hii ni lugha ya picha inayoelezea hisia kali walizokuwa nazo walipokuwa wakiongea na Yesu. Tafsiri mbadala: "Tulikuwa na hisia kali alipokuwa akiongea na sisi."

wakati alipotufungulia maandiko

Yesu hakufungua kitabu au gombo la chuo. Tafsiri mbadala: "wakati alipokuwa akituelezea maandiko.

Luke 24:33

Wakanyanyuka

Inahusiana na wale watu wawili

nyanyuka

"kuamka" au "kusimama"

wale kumi na moja

Hii inaongelea wale mitume wa Yesu. Yuda hakuwa pamoja nao.

wakisema, "Bwana amefufuka kwelikweli

Wale mitume kumi na moja na wale waliokuwa pamoja nao walisema hivyo.

Hivyo wakawaambia

"Hivyo wale watu wawili wakawaambia"

mambo yaliyotokea njiani

Hii inamaanisha Yesu alivyowatokea wakiwa njiani kuelekea kijiji cha Emmau.

namna Yesu alivyodhihirishwa kwao

Tafsiri mbadala: "namna walivyomtambua Yesu"

katika kuumega mkate

"wakati Yesu alipouvunja mkate" au "wakati Yesu alipouchana mkate"

Luke 24:36

Yesu mwenyewe

Neno "mwenyewe" linakazia juu ya Yesu na mshangao wa Yesu kiuhakika kuwatokea. Wengi wao walikuwa hawajamuona baada ya ufufuko wake.

katikati yao

Tafsiri mbadala: "mahali ambapo wote wanaweza kumuona"

Amani iwe kwenu

"Basi iweni na amani" au "Basi Mungu awape amani!"

waliogopa na kujawa na hofu

"walishikwa na mshangao na kuogopa"

wakafikiri kwamba waliona roho

Walikuwa hawajaelewa kiuhalisia kwamba Yesu kwelikweli yu hai.

roho

Hapa inamaanisha roho ya mtu aliyekufa.

Luke 24:38

Kwa nini mnafadhaika?

Yesu anatumia swali kuwatia moyo. Tafsiri mbadala: "Msiogopeshwe."

Kwanini maswali yanainuka mioyoni mwenu?

Yesu anatumia swali kuwakemea kidogo. Yesu alikuwa anawaambia wasitie mashaka kwamba yu hai. Tafsiri mbadala: "Msitie mashaka katika akili zenu!" au "Acheni kutia mashaka!"

nyama na mifupa

Hii ni namna ya kumaanisha mwili

Luke 24:41

bado na furaha iliyochanganyikana na kutokuamini

"bado hawakuweza kuamini kwamba ni ukweli kabisa." Walikuwa na furaha sana, lakini wakati huohuo, ilikuwa ngumu kwao kuamini kwamba ni kweli kabisa imetukia.

na kustaajabu

"na walishangazwa" au "na kustaajabu hili laweza kutokeaje"

mbele yao

"mbele yao" au "wakiwa wanatazama"

Luke 24:44

Nilipokuwa nanyi

"Wakati bado nilipokuwa nanyi"

yote yaliyoandikwa kwenye sheria ya Musa na manabii na zaburi

Tafsiri mbadala: "yote ambayo Musa, manabii, na waandishi wa Zaburi waliandika kuhusu mimi"

lazima yatimilike

Tafsiri mbadala: "Mungu atayatimiliza" au "Mungu atayafanya yatokee"

Luke 24:45

Kisha akafungua akili zao, kwamba waweze kuyaelewa maandiko.

Tafsiri mbadala: "Kisha akawawezesha kuyaelewa maandiko"

Kwamba imeandikwa

Tafsiri mbadala: "Hivi ndivyo watu hapo zamani waliandika"

siku ya tatu

"baada ya usiku mbili"

toba na msamaha wa dhambi lazima ihubiriwe

Tafsiri mbadala: "wafuasi wa Kristo inawapasa kuhubiri kwamba watu wanahitaji kutubu ili Mungu awasamehe dhambi zao"

kwa jina lake

Tafsiri mbadala: "kama wawakilishi wake" au "na mamlaka yake"

mataifa yote

"makabila yote kwenye jamii" au "makundi yote ya watu"

Luke 24:48

Ninyi ni mashahidi

"Mnatakiwa kuwaambia wengine kwamba mliyoyaona kuhusu mimi ni kweli." Wanafunzi walikuwa wameyaona maisha ya Yesu, kufa kwake, kufufuka kwake, na waliweza kueleza kwa wengine kitu gani alifanya.

Nawapelekea ahadi ya Baba yangu juu yenu

"Nitawapa kile ambacho Baba yangu aliahidi kuwapa." Yesu, Mungu Mwana, atatoa kile Mungu Baba alikiahidi kwa wafuasi wake wote, ambacho ni Mungu Roho Mtakatifu.

Baba

Hiki ni cheo muhimu kwa Mungu

mtakapovishwa nguvu

Nguvu ya Mungu itawafunika kwa namna ileile nguo inavyomfunika mtu. Tafsiri mbadala: "mnapokea nguvu."

kutoka juu

"kutoka juu" au "kutoka kwa Mungu"

Luke 24:50

Ikatokea

"Ilitokea"

alipokuwa akiwabariki

"wakati Yesu alipokuwa anamuomba Mungu kuwatendea mema"

akabebwa

Kwa sababu Luka haelezei kiuwazi nani alimbeba Yesu kwenda juu, hatujui kama alikuwa Mungu mwenyewe au malaika mmoja au malaika wengi.

Luke 24:52

Taarifa za jumla:

Mistari hii inaelezea matendo ya Mitume

walimwabudu yeye

"Mitume walimwabudu Yesu"

na kurudi

kisha walirudi

waliendelea kubaki hekaluni

hii inamaanisha kuwa walienda hekaluni kila siku

hekaluni

makuhani peke yao ndio waliruhusiwa kuingia hekaluni

wakimbariki Mungu

wakimsifu Mungu

Utangulizi wa injili ya Yohana

Sehemu ya 1: Utangulizi wa Ujumla

Maelezo ya Injili ya Yohana

  1. Utangulizi kuhusu Yesu ni nani (1:1-18)

  2. Yesu anabatizwa, na kuwachagua wanafunzi kumi na wawili (1:19-51)

  3. Yesu anahubiri, anafundisha, na kuwaponya watu (2-11)

  4. Siku saba kabla ya kifo cha Yesu (12-19

  5. Yesu anafufuka (20:1-29)

  6. Yohana anasema kwa nini aliandika injili yake (20:30-31)

  7. Yesu anakutana na wanafunzi (21)

Je, kitabu cha Yohana kinahusu nini?

Injili ya Yohana ni moja ya vitabu vinne katika Agano Jipya ambavyo huelezea baadhi ya maisha ya Yesu Kristo. Waandishi wa Injili waliandika juu ya mambo mbalimbali kuonyesha kuwa Yesu alikuwa nani na ni nini alichofanya. Yohana alisema kwamba aliandika injili yake "ili watu waweze kuamini kwamba Yesu ndiye Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai" (20:31).

Injili ya Yohana ni tofauti kabisa na Injili nyingine tatu. Yohana hajumuishi baadhi ya mafundisho na matukio ambayo waandishi wengine walijumuisha katika injili zao. Pia, Yohana aliandika juu ya baadhi ya mafundisho na matukio ambazo hazipo katika injili nyingine.

Yohana aliandika mengi juu ya ishara alizofanya Yesu ili kuthibitisha kwamba kile Yesu alisema juu yake mwenyewe ni kweli. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sign)

e, kichwa cha kitabu hiki kinapaswa kutafsiriwaje?

Watafsiri wanaweza kuchagua kuita kitabu hiki kwa kichwa chake asilia, "Injili ya Yohana" au "Injili kama ilivyoandikwa na Yohana." Au wanaweza kuchagua kichwa ambacho kinaweza kuwa wazi, kama vile "Habari Njema Kuhusu Yesu ambayo Yohana Aliandika." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-names)

Nani aliandika Kitabu cha Yohana?

Kitabu hiki hakitupi jina la mwandishi. Hata hivyo, tangu wakati wa Kikristo wa kwanza, Wakristo wengi wamefikiri kwamba Mtume Yohana ndiye aliyekuwa mwandishi.

Sehemu ya 2: Dhana muhimu za Kidini na za desturi

Kwa nini Yohana anaandika mengi kuhusu wiki ya mwisho ya maisha ya Yesu?

Yohana aliandika mengi kuhusu wiki ya mwisho ya Yesu. Alitaka wasomaji wake kufikiri sana juu ya wiki ya mwisho ya Yesu na kifo chake msalabani. Alitaka watu waelewe kwamba Yesu kwa hiari alikufa msalabani ili Mungu awasamehe kwa ajili ya kutenda dhambi. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

Sehemu ya 3: Masuala muhimu ya Tafsiri

Maneno "kubaki," "kuishi," na "kukaa" yana maana gani katika injili ya Yohana?

Mara nyingi Yohana alitumia maneno "kubaki," "kuishi", na "kukaa" kama mifano. Yohana alizungumuza juu ya mwamini kuwa mwaminifu zaidi kwa Yesu na kumjua Yesu vizuri kama neno la Yesu "lilibaki" ndani ya yule mwamini. Pia, Yohana alizungumuza juu ya aliyejiunga kiroho na mtu mwingine kwa kusema "alibaki" ndani yake. Wakristo wanasema "kubaki" katika Kristo na kwa Mungu. Baba anasemwa "kubaki" ndani ya Mwana, na Mwana anasemwa "kubaki" ndani ya Baba. Mwana anasemwa "kubaki" katika waumini. Roho Mtakatifu pia anasemwa "kubaki" ndani ya waumini.

Watafsiri wengi wataona vigumu kwa kutafsiri mawazo hayo katika lugha zao kusema maneno sawasawa kabisa. Kwa mfano, Yesu alitaka kuelezea wazo la Mkristo kuwa kiroho pamoja naye wakati aliposema, "Yeye anayekula mwili wangu na kunywa damu yangu anakaa ndani yangu, na mimi ndani yake" (Yohana 6:56). UDB hutumia wazo la "ataunganishwa na mimi, nami nitaunganishwa naye." Lakini watafsiri wanaweza kutumia maneno nyingine za kueleza wazo hilo.

Katika kifungu hicho, "Ikiwa maneno yangu yanakaa ndani yenu" (Yohana 15:7), kulingana na UDB wazo hili linatafsiriwa kama, "Ikiwa unaishi katika ujumbe wangu." Watafsiri wanaweza kutumia tafsiri hii kama mfano.

Je, kuna maswali makuu gani katika maandishi ya Kitabu cha Yohana?

Haya ni masuala muhimu zaidi ya maandishi katika Kitabu cha Yohana:

Watafsiri wanashauriwa kutotafsiri kifungu hiki. Hata hivyo, ikiwa katika eneo la watafsiri, kuna matoleo ya zamani ya Biblia ambayo yanajumuisha kifungu hiki, basi watafsiri wanaweza kukijumuisha. Ikiwa inatafsiriwa, inapaswa kuwekwa ndani ya mabano ya mraba ([]) ili kuonyesha kwamba labda asili yake sio Injili ya Yohana. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/jit.html#translate-textvariants)

Kifungu hiki kinajumuishwa katika matoleo mengi ya kale na ya kisasa ya Biblia. Lakini hakiko katika nakala za kwanza za Biblia. Watafsiri wanashauriwa kutafsiri kifungu hiki. Kinapaswa kuwekwa ndani ya mabano ya mraba ([]) kuonyesha kwamba labda asili yake sio Injili ya Yohana. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/jit.html#translate-textvariants)

"kupitia katikati yao, na hivyo kupitia" (8:59)

Lakini ni hakika kwamba kifungu hiki hakikuwa hapo awali kwa Injili ya Yohana. Hakipaswi kuingizwa. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/jit.html#translate-textvariants)

(See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/jit.html#translate-textvariants)

John 1

Yohana 01 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri hupendelea kuweka mbele kidogo nukuu za Agano la Kale. ULB na tafsiri nyingine nyingi za Kiingereza huingiza mistari ya 1:23, ambayo ni nukuu kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

"Neno"

Hili ni neno la kipekee unaotumiwa kumtaja Yesu. Yeye ni "Neno la Mungu" katika hali ya kimwili na ufunuo wa mwisho wa Mungu mwenyewe duniani. Ingawa hii inaweza kuonekana kuwa mafundisho magumu, ni rahisi sana: Yesu ni Mungu, aliyeumba mbingu na dunia. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#wordofgod, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#flesh, and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#reveal)

Mwanga na Giza

maneno haya ni mifano ya kawaida katika Agano Jipya. Mwangaza hutumiwa hapa ili kuonyesha ufunuo wa Mungu na haki yake. Giza ni mfano wa dhambi na dhambi hupenda kufichwa kwa macho ya Mungu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#light, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#darkness and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

"Watoto wa Mungu"

Wakati watu wanpomwamini Yesu, wanaacha kuwa "watoto wa ghadhabu" na kuwa "watoto wa Mungu." Wanaingizwa katika "familia ya Mungu." Huu ni mfano muhimu ambayo itafunuliwa katika Agano Jipya. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#believe and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#adoption)

Mifano muhimu za usemi katika sura hii

Mifano

Ingawa vitabu vingine vya Injili mara nyingi vinatumia mifano katika mafundisho ya Yesu na katika unabii, sura ya kwanza ya injili hii inatumia mifano kwa kielelezo cha maana ya maisha ya Yesu. Kwa sababu ya mifano hizi, msomaji anaonyeshwa kwamba injili hii italeta ufahamu zaidi juu ya maisha ya Yesu kwa kitheolojia. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Mwanzoni kulikuwa neno"

Sehemu ya kwanza ya sura hii inafuata taratibu ya kanuni za ufahamuna muundo wa kishairi. Kutafsiri taratibu hizi itakuwa vigumu sanai.

"Mwana wa Binadamu"

Yesu anajiita mwenyewe kama "Mwana wa Binadamu." Lugha zingine haziwezi kuruhusu mtu kujitaja mwenyewe kama 'mtu wa tatu.' (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sonofman)

| >>

John 1:1

Hapo mwanzo

Ina maanisha mwanzoni kabisa ya wakati kabla Mungu hajaumba mbingu na nchi.

Neno

Iina maanisha Yesu. Kama inawezekana litafsiri kama "Neno" Kama katika lugha yako "Neno" ni ngeli ya kike, inawe kufasiriwa kama "yule anayeitwa "Neno."

Vitu vyote viliumbwa kwa yeye

Hii inaweza kufasiriwa katika hali tendaji. "Mungu alivifanya vitu vyote kwa yeye."

pasipo yeye hakuna hata kitu kimoja kilichofanyika ambacho kilichofanyika.

Hii inaweza kufasiriwa katika hali tendaji. "Mungu hakufanya kila kitu chochote pasipo yeye" au " Mungu alifanya vitu vyote akiwa naye."

John 1:4

Ndani yake kulikuwa uzima

Hapa "uzima"ni mfano kwa kusababisha kila kitu kuishi. A: "Yeye anayeitwa Neno ndiye aliyesababisha kila kitu kuishi.

Uzima

hapa tumia neno la jumla kwa "uzima." Kama utatafasiri moja kwa moja unaweza kufasiri kama "uzima wa kiroho".

Uzima huo ulikuwa nuru ya wanadamu wote

"Nuru" ni mfano ambao ambao unamaanisha ufunuo wa Mungu.AT: aliifunua kweli kwetu kama vile nuru ifunuavyo kile kilichomo gizani.

NUru yang'ara gizani wala giza halikuliweza

Kama vile ambavyo giza lisivyoweza kuizima nuru, watu wabaya hawajaweza kumzuia yeye ambaye ni kama nuru katika kuifunua kweli ya Mung.

John 1:6

Kuishuhudia nuru

Hapa "Nuru" ni mfano kwa ajili ufunuo wa Mungu katika Yesu. AT: "onyesha jinsi ambavyo Yesu alivyo kama nuru halisi kutoka kwa Mungu."

John 1:9

Niru ya kweli

Hapa "nuru" ni mfano ambao unamwakilisha Yeus kama ufunuo wa kweli kutoka kwa Mungu.

hutia nuru

"hutoa nuru kwa"

John 1:10

Alikuwapo duniani, na kwa yeye ulimwengu ulipata kuwepo, lakini ulimwengu haukumjua

AT: "Lakini pamoja kwamba alikuwa ulimwenguni, na kwamba Mungu aliumba vitu vyote kwa yeye, bado watu hakumtambua."

alikuja kwa vitu vyake, na watu wake hawakumpokea

AT: "Alikuja kwa wenzake , na wenzake hwakumpokea."

John 1:12

Amini juu ya

Hii ina maanisha Yesu kuwa Mwokozi na kuishi kwa jinsi ambayo inamtukuza.

Jina

Neno 'jina" ni neno ambalo linaelezea utamblisho wa "Yesu" na kila kitu kitu kuhusu yeye.

aliwapa uwezo

aliwapa mamlaka" au "aliwezesha kwa ajili yao"

Wana wa Mungu

Neno "watoto"ni mfano ambao unawakilisha uhusiano wetu na Mungu, ambao ni kama vile watoto na baba.

John 1:14

Neno

Huu ni mfano ambao unamaanisha kwa Yesu. Yeye ndiye aliye mfunua Mungu alivyo.

Baba

Hiki ni cheo muhimu kwa cha Mungu.

amejaa neema

AT: "ambaye mara zote hufanya kwa wema kwa ajili yetu katika njia mbazo hatustahili."

yeye ajaye baada yangu

Yohana anaongea kuhusu Yesu. Neno "anakuja baada yagu" linamaanisha kwamba huduma ya Yohana ilikuwa tayari imeanza na huduma ya Yesu itaanza baadaya, baada ya Yohana.

ni mkuu kuliko mimi

"ni mkuu zaidi yangu" au" ni muhimu zaidi"

kwa sababu amekuwapo kabla yangu

Kuwa mwangalifu usitafsiri kwamba Yesu ni wa muhimu zaidi kwa sababu ni mzee kuliko Yohana. Yesu ni mkuu zaidi ya Yohana kwa sababu yeye ni Mungu Mwana, ambaye amekuwepo na kutawala juu ya vitu vyote pamoja na Mungu.

John 1:16

utimilifu

Huli neno linamaanisha kwa neema ya Mungu ambayo haina mwisho.

kipawa cha bure baada ya kingine

"baraka baada ya baraka"

aliye mwanadamu pekee, ambaye ni Mungu

Hii inaweza kumaanisha1)aliye Mungu wa wa pekee" au" 2) yeye aliye Mwana wa pekee,"

aliye katika kifua cha Baba

Neno "kifua" ni mfano . Hii inamaanisha kuwa Yesu ndiye aliye karibu na Baba" ikimaanisha ushusino wa karibu.

Baba

Hiki ni cheo muhimu cha Mungu.

John 1:19

Wayahudi walitumwa kwake kutoka Yerusalemu

Hapa mwandishi anatumia mfano. Neno "Wayahudi" limetumika kwa kuwakilisha "Viongozi wa Kiyahudi." AT:" Viongozi wa Kiyahudi waliwatuma kwake kutoka Yerusalemu.

Yeye alisema wazi, wala hakukana

Neno la pili linaeleza maneno hasi ambayo neno la kwanza linachokisema katika mtazamo chanya. Hii inasisitiza kuwa Yohana alikuwa akisema kweil.AT: "Aliwambia ukweli bila woga".

U nani?

AT: "U nani ni kama sio Masihi"? au " Nini kinachoendelea?" au " Unafanya nini."

John 1:22

Kiunganishi cha sentesi:

Johana anaendela kuongea na makuhani na walawi.

wakamwambia

"makuhani na Walawi wakamwambia Yohana>"

sisi...sisi

Makuhani na Walawi, sio Yohana.

Akasema

"Yohana akasema"

Mimi ni sauti aliaye nyikani

Neno "sauti" ni mfano ambao unamwakilisha Yohana na ujumnbe wake. AT: Mimi ni kama mtu ongea kwa sauti mbapo hakuna mtu yeyote anaweza kunisikia.

Inyosheni njiai ya Bwana

Hapa neno "njia" limetumika kama mfanoAT: Jiandae mwenyewe kwa ajili ya ujio wa Bwana kama vile ambavyo watu waandaavyo barabara kwa ajili ya ujio wa mtu muhimu.

John 1:24

Basi kulikuwa na mtu ametumwa kutoka kwa Mafarisayo

Haya ni habari ya nyuma kuhusu watu waliomuuliza Yesu kutoka kwa Mafarisayo.

John 1:26

Maelezo kwa jumla:

mstari wa 28 unatwambia habari za nyuma kuhusu mwanzo wa hadithi.

Huyu ndiye ajaye baada yangu

AT: " Atawahubiri baada ya mimi kuondoka"

Mimi sisitahili "kufungua gidamu ya viatu vyake

kazi ya kufungua viatu vyake " ambayo ni kazi ya mtumwa au mja kazi ni fumbo. Johana nasema kuwa hasitahili kumfanyia Yesu kazi hata ile ya chini kabisa liyofanywa na watumwa.

John 1:29

Mwanakondoo wa Mungu

Huuu ni mfano ambao unawakilisha Utimilifu wa dhabihu kamilifu ya Mungu. Yesu anaitwa "Mwanakondoo wa Mungu" kwa sababu alikuwa dhabihu kwa ajili ya dhambi za watu.

dunia

neno "dunia" ni neno ambalo linalojumuisha watu wote duniani.

ajaye nyuma yangu, ni mkuu, kwa maana amekuwapo kabala yangu

Tafsili hili kama ulitafsiri 1:14:1:15

John 1:32

shuka

"shuka chini"

kama njiwa

hili ni neno lenye lugha ya picha . "Roho " anashuka chini kama vile ambavyo njiwa ashukavyo kwa mtu.

mbinguni

Neno "mbingu" linamaanisha "anga."

Mwana wa Mungu

Baadhi ya nakala za kifungu hiki husema "Mwana wa Mungu": wengine husema " mchaguliwa wa Mungu."

Mwana wa Mungu

Hiki ni cheo muhimu kwa Yesu, Mwana wa Mungu.

John 1:35

Tena, siku iliyofuata

Hii ni siku nyingine. Ilikuwa ni siku ya pili Yohana alipomwona Yesu.

Mwanakondoo wa Mungu

Huu ni mfano ni mfano ambao unawakilisha dhabihu timilifu. Yesu ni Mwanakondoo wa Mungu kwa sababu alidhabihiwa kulipa dhambia za watu.

John 1:37

muda wa saa kumi

Neno linaonyesha wakati wa mchana, kabla ya giza, ambao usinge ruhusu kusafiri kwenda katika mji mwingine, yawezekana 10 za jioni.

John 1:40

Maelezo kwa Ujumla:

Mistari hii utupa maelezo kuhusu Andrea na jinsi alivyomleta ndugu yake Petro kwa Yesu. Hii ilitokea kabla hajaenda mahali ambapo Yesu alikuwa akikaa.

mwana wa Yohana

Huyu ni Yohana Mbatizaji. " Yohana lilikuwa jina la kawaida.

John 1:43

Basi Filipo alikuwa mtu wa Bethsaida, mji wa Andrea na Petro

Hii ni habari ya nyuma kuhusu Filipo.

John 1:46

Nathanaeli akamwambia

"Nathaneli akamwambia Filipo."

Je jambo jema laweza kutoka Israeli?

Neno hili lijitokeza kama swali kuonyesha msisitizo.AT: "Hakuna kitu kizuri kinaweza kutoka Nazarti."

ambaye ndani yake hakuna udanganyifu

Hili linaweza kusema katika mtazamo chanya. AT: "mtumkweli aliyekamilika."

John 1:49

Rabbi, wewe ni Mwana wa Mungu! Wewe ni mfalme wa Israeli!

Nathanaeli anasema Yesu ni "Mwana wa Mungu" kwa sababu Yesu amjua Nathanaeli pasipo kukutana naye awali.

Mwana wa Mungu

Hiki ni cheo muhimu kwa Yesu.

Kwa sababu nilikuambia.. je unaamini?

Hili jibu linaonekana katika jinsi ya swali kuonesha msisitizo. unaweza kuifasili kama sentesi. AT: "Unaamini kwa sababu nilisema, nilikuona chini ya mtini'!

Amini, amini

Tafsiri hili jinsi ambavyo lugha yako inavyosisitiza kuwa kile kinachofuata ni kweli.

John 2

Yohana 02 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Divai

Ilikuwa ni desturi ya divai kutumiwa wakati wa sherehe. Haikuchukuliwa uovu kunywa divai.

Kuwafukuza wanaobadili pesa

Hii ndiyo maelezo ya kwanza juu ya Yesu kuwafukuza nje ya hekalu wanaovunja pesa. Tukio hili lilionyesha mamlaka ambayo Yesu alikuwa nayo juu ya hekalu na juu ya Israeli yote.

"Alijua yaliyokuwa ndani yao"

Yohana anajua kwamba inawezekana kwa Yesu kuwa na aina hii ya ujuzi kwa sababu tu ya Yesu kuwa Mungu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Wanafunzi wake wakakumbuka"

Maneno haya hutumiwa kama ufafanuzi wa matukio yanayotokea katika sura hii. Maneno haya hayajulikani wakati ambapo matukio hutokea, lakini yamejulikana wakati kitabu kilipoandikwa. Watafsiri wanaweza kuchagua kutumia mabano ili kutenga maelezo au ufafanuzi wa mwandishi juu ya matukio yaliyopita.

<< | >>

John 2:1

Maelezo kwa Jumla:

Yesu na wanafunzi wake walikuwa wamealikwa arusini. Mstari huu unaonyesha habari ya nyuma juu ya habari inavyoanza.

Siku tatu baadaye

Wafaasili wengi husoma hili kama siku ya tatu baada ya Yesu kumwiita Filipo and Nathanaeli kuja kwake. Siku ya kwanza inaonekana katika Yohana 1:35 na siku ya pili ni 1:43

Yesu na wanafunzi wake walikuwa wamealikwa harusini

Hii inaweza kutamkwa kama tendaji. AT: " Mtu alimwalika Yesu na wanafunzi wake katika arusi."

John 2:3

Mwanamke

Hii inaa mweelezea Mariamu. Kama ni neno lenye ukakasi katika lugha yako kwa mwana kumwiita mama mwanamke, tumia neno jingine.

hiyo inanihusu nini?

Hili linaonekana katika muundo wa swali ili kuonesha msisitizo . unaweza kukuifasili kama sentensi. AT: " hii haimaanishi kufanya nami" au " usiniambie nini cha kufanya."

Muda wangu bado haujatimia

Neno "muda" ni neno ambalo inawakilisha kuwa tukio maalumu kwa Yesu kuonesha kwamba yeye ni Masihi kwa miujiza.AT: "Sio muda mwafaka kwangu kufanya matengo makuu."

John 2:6

nzio mbili hadi tatu

"lita 80 hadi 120." nzio moja lilikuwa was

hadi juu

hii inamaanisha "juu sana' au "iliyojaa kabisa."

mhudumiaji mkuu

Hii ina maanisha mtu aliye na mamlaka juu ya chakula na kinywaji.

John 2:9

(lakini watumishi waliochota maji walifahamu)

hii ni habari ya nyuma.

kulewa

kutokuweza kuelewa pombe ghali na isiyo ghali kwa sababu ya kunywa kiasi kingi cha kileo.

John 2:11

Viunganishi vy maneno:

Hii si mwenendelezo wa hadithi kuu, badala yake inashamilisha hadithi.

Kana

Jina la sehemu

akifunua utukufu wake

Hapa "utukufu" ni neno linaonesha nguvu za Yesu.

John 2:12

akateremka

Hii inamaanisha kwamba walisafiri kutoka sehemu ya mwinuko kuelekea bondeni. Kana in kusini magaharibi ya Kaperanaumu na iko juu.

ndugu zake

Neno "ndugu"linajumisha kaka na dada. Kaka na dada wa Yesu walikuwa wadogo kuliko alivyokuwa.

John 2:13

Maneno ya jumla:

Yesu na wanafunzi wake wanapanda kwenda Yerusalemu kwenye hekalu.

juu hadi Yerusalemu

Hii inamaasha kuwa walisafiri kutoka kwenye mwinuko kwenda chini. Yerusalemu imejengwa juu ya kilima.

ndani ya hekalu

inamaanisha sehemu ya nje ya hekalu mahali ambapo wasio wayahudi waliruhusiwa kuabudu.

wale waliouza

watu waliweza kununua hekaluni na kuwadhabihu kwa ajili ya kumuheshimu Mungu.

wabadili fedha

Mamlaka ya Kiyahudi iliitaji watu ambao walihitaji kununua wanyama kwa ajili ya dhabihu kubadilisha pesa zao kutoka kwa wabadilishaji wa fedha.

John 2:15

Basi

Neno hili linaonyesha tukio lililotokea kwa sababu ya kile kilichotokea mwanzoni. Katika hali hii, Yesu aliwaona wabadili fedha wamekaa katika hekalu.

Acheni kuifanya nyumba ya Baba yangu soko

Yesu, Mwana wa Mungu, anawafukuza wafanyabiashara kutoka mahali palipoandaliwa kwa ajili ya ibada ya Baba yake, Mungu Baba, kumuheshimu.

nyumba ya Baba yangu

Haya ni maneno ambayo Yesu aliyasema yakimaanisha hekalu.

Baba

Hiki ni cheo muhimu kwa Mungu.

John 2:17

iliandikwa

Hii inaweza kusema katika muundo wa kutenda. Kuna mtu alikuwa ameandika."

nyumba yako

Neno hili linamaanisha, nyumba ya Mungu.

maliza

Neno hili "maliza" linaelekeza kwenye "moto." Upendo wa Yesu kwa ajili ya hekalu ni kama moto unaowaka ndani yake.

ishara

Hili ni tendo ambalo linalothibitisha kuwa ni jambo la kweli.

mambo haya

Haya yanamaanisha matendo ya Yesu aliyokuwa kinyume na wabadili fedha ndani ya hekalu.

Livunjenihili hekalu, na nitaliinua baada ya siku tatu

Yesu anamaanisha mwili wake kama hekalu kwamba atakufana kwamba atakuwa mzima tena baada ya siku tatu. Lakini, ni muhimu kutafasili haya maneno kuwa yameelezwa kuelezea kuvunja na kujenga jengo. Yesu hawaamuru wanafunzi wake kuvunja jengo la hekalu.

nitaliinua

Hii inamaanisha "kujenga" au 'kurudisha"

John 2:20

Yohana 2: 20- 22

Maelezo ya jumla: ilichukuwa miaka arobaini na sita...utaijenga kwa siku tatu? Miaka arobaini na sita... siku tatu aliamini/ waliamini hii sentesi

John 2:23

Basi alikuwa Yerusalemu

Neno basi linatutambulisha katika tukio jingine katika hadithi

wakaalimini jina lake

Hapa "jina" ni neno linalowakilisha utu wa Yesu. "aminini" au "kuamini katika yeye."

ishara za maajabu

Miujiza inaweza kuitwa "ishara" kwa sababu yanatumiwa kama ushahidi kwamba Mungu ni mwenye nguvu ambaye aliye na mamlaka kamili juu ya dunia.

John 3

Yohana 03 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Mwangaza na Giza

Hizi ni taswira za kawaida katika Agano Jipya. Mwangaza hutumiwa hapa ili kuonyesha ufunuo wa Mungu na haki yake. Giza linaelezea dhambi na dhambi hubakia kufichwa kwa macho ya Mungu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#light, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#darkness and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Tunajua kwamba wewe ni mwalimu anayetoka kwa Mungu"

Ingawa hii inaonekana kuwa inaonyesha imani, sivyo. Sababu kumwamini Yesu kama "mwalimu tu" inaonyesha ukosefu wa ufahamu wa kuwa yeye hakika ni nani. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

"Mwana wa Binadamu"

Yesu anajiita mwenyewe kama "Mwana wa Binadamu." Lugha zingine haziwezi kuruhusu mtu kujitaja mwenyewe kama 'mtu wa tatu.' (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sonofman)

<< | >>

John 3:1

Maneno kwa Ujumla:

Nikodemo anakuja kumwona Yesu.

sasa

Neno hili lintumika hapa kutambulisha sehemu nyingine ya hadithi na kumtambulisha Nikodemo.

mjumbe

sehemu ya kundi

Halimashauli ya Wayahudi

hHalimashauli ya Kiyahudi inaitwa "Sanihedrini." Hili lilikuwa ndilo baraza muhimu kwa mabaraza yote ya Kiyahudi.

twafahamu

hapa "sisi" linajumuisha, likimaanisha tu kwa Nikodemo na wanachama wengine wa halimashauli ya Kiyahudi.

John 3:3

Kiunganishi cha sentesi:

Yesu na Nikodemo wanaendelea kuongea.

Amini, amini

Tafsiri haya kama ulivyotafsiri 1:49; 1:51.

zaliwa mara ya pili

"kuzaliwa kutoka juu" au kuzaliwa na Mungu."

ufalme wa Mungu

Neno "ufalme" ni mfano kwa utawala wa Mungu." 'Sehemu ambayo Mungu anatawala."

Je mtu anaweza kuzaliwa awapo mzee?

Nikodemo alitumia swali hili kusisitiza kwamba hili lisingelitokea. "Ni kweli mtu hawezi kuzaliwa tena wakati akiwa mzee!"

Hawezi kuingia tumboni mwa mama yake mara ya pili ili azaliwe, je anaweza kufanya hivyo?

Pia Nikodemo anatumia swali hili kusisitiza imani yake kuwa imani yake kuwa kuzaliwa mara ya pili ni jambo lisilowezekana." Ni kweli, hawezi kuingia tumboni mwa mama yake mara ya pili!"

mara ya pili

"tena"au "mara mbili"

tumbo

sehemu ya tumbo la mwanamke ambapo mtoto hukulia.

John 3:5

amezaliwa kwa maji na kwa roho

kuna maana mbili: 1)"kubatizwa ndani ya maji na katika Roho" au 2)"kuzaliwa kimwili na kiroho"

Amini, amini

unaweza kufasiri mane haya kama yalivyotumika katika tafsiri za hapo mwanzo.

ufalme wa Mungu

Neno "ufalme" ni fumbo kwa ajili ya utawala wa Mungu katika maisha ya mtu.

John 3:7

Kiunganishi cha Sentesi:

Yesu anaendelea kuongea na Yesu.

Ni lazima uzaliwe mara ya pili

"unapaswa kuzaliwa kutoka juu"

upepo huvuma popote upendako

Katika lugha ya mwanzo, maneno. upepo na Roho ni maneno sawa. Mwongeaji anamaanisha upepo kama ni mtu. "Roho Mtakatfu ni kama upepo ambao unavuma popote upendapo."

John 3:9

Mambo haya yanawezekanaje?

hili ni swali mbalaga ambalo linalosisitiza sentesi. "Hii hawezekani!" au" Hili haliwezi kutokea!"

Wewe ni mwalimu wa Israeli na hauyajui mambo haya?

Hili ni swali mbagala ambalo linaonyesha msisitizo. "weweni mwalimu wa Israeli , na ninashangaa kwamba haufahamu maneno haya!"

Amini, amini

Tafsiri kama ulivyotafsiri.

twazungumza

Yesu aliposema "sisi' hakuwa anamjumuisha Nikodemo.

John 3:12

Kiunganishi cha Maneno:

Yesu anamjibu Nikodemo

mtawezaje kuamini kama nitawaeleza mambo ya mbinguni?

katika sehemu "wewe" ni umoja.

mtawezaje kuamini kama nikiwambiamambo ya mbinguni

"Hautaamini kama nikiwambia mambo ya mbinguni."

mbinguni

hii inamaanisha mahali ambapo Mungu anaishi.

John 3:14

Kama vile Musa alivyomwinua juu yule nyoka jangwani

hili ni fumbo baadhi ya watu "watainua" Yesu kama Musa alivyoinuliwa nyoka wa shaba katika jangwa.

Vivyo hivyo Mwana wa Adamu ni lazima ainuliwe juu

Jangwani ni sehemu kavu lakini hapa anamaanisha mahali walipotembea Musa na Waisraeli.

katika jangwa

Jangwani ni sehemu kavu, sehemu ya jangwa, lakini hapa wanamaanisha mahali ambapo Musa na Waisraeli walizunguka."

John 3:16

Mungu aliupenda ulimwengu

Neno "dunia" hapa ni neno linalojumuisha kila kitu duniani.

alipenda

hii ni aina ya upendo ambao unatoka kwa Mungu na unatakia mema wengine, hata kama mtu hanufaiki. Mungu mwenyewe ni upendo na ndiye chanzo cha upendo wa kweli.

mwana wa pekee

"mmoja na Mwana wa pekee"

kwa sababu Mungu hakumtuma mwana ulimwenguni ili auhukumu, bali ulimwengu uokolewe kwa yeye

maneno mawili yanaweza kuwa yanamaanisha na yametajwa mara mbili ili kwamba kusisitiza kwanza katika mtazamo hasi na chanya. Baadhi ya lugha inaweza kuonyesha msisitizo kwa namna nyingine. Kusudu la Mungu kumtuma Mwanae ni kwamba ulimwengu uokolewe katika yeye.

ahukumiwi

anachiwa huru

hukumu

adhibu

Mwana wa Mungu

Hiki ni cheo muhimu kwa Yesu.

John 3:19

Kiunganishi cha Sentesi:

Yesu anamaliza kumjibu Nikodemo.

nuru imekuja ulimwenguni

Neno "nuru" ni fumbo kwa kweli ya Mungu iliyofunuliwa katika Yesu. Dunia ni neno linalojumisha vitu vyote vilivyomo duniani. Yeye ambaye ni kama nuru ameifunua kweli ya Mungu kwa watu."

watu wakalipenda giza

"giza" ni fumbo linalomaanisha mahali ambapo hawajapokea nuru" ya ufunuo wa Mungu katika Kristo.

ili kwamba matendo yake yasiwe dhahili

inaweza kutamkwa katika muundo wa kutenda. "ili kwamba nuru isioneshe mambo ayafanyayo" au " kwamba ili nuru isifunue matendo yao.

matendo yake yaonekane wazi

Hili linaweza kutamkwa katika muundo tenda. " Watu wanaweza matendo yake" au "kila mtu aweze kuona mambo ahafanyayo.

John 3:22

Baada ya haya

Hii inamaanisha baada ya Yesu kuongea na Nikodemo.

Aenoni

Neno hili linamaanisha "chemuchemi."

Salimu

kijiji au mji ulio karibu na Mto Yorodani.

kwa sababu mahali pale kulikuwa na maji mengi

"kwa sababu kilikuwa na chemuchemi nyingi katika sehemu ile."

walikuwa wakibatizwa

hili linaweza kusemwa kwa muundo wa kutenda. '" Yohana alikuwa akiwabatiza " au " alikuwa akiwabatiza."

John 3:25

kukatokea malalamiko baina ya baadhi ya wanafunzi wa Yohana na Myahudi

"Tena wanafunzi wa Yohana na Myahudi wakaanza kubishana.

kutoelewana

kugombana kwa maneno

tazama, anabatiza

Katika sentesi hii "tazama" ni amri ikimaanisha tilia manani!" " Tazama! Anabatiza" au " Tazama! anabatiza."

John 3:27

Mtu hawezi kupokea kitu chochote isipokuwa

"Hakuna mtu aliye na nguvu isipokuwa"

amepewa kutoka mbinguni

Neno "mbinguni" likimaanisha Mungu. Hili linaweza kuchukuliwa katika muundo tenda. " Mungu amempa."

ninyi wenyewe

ninyi ni kwa wingi na inamaanisha watu wote ambao Yohana anazungumza nao.

nimetuma mbele zake

"Mungu amenituma kufika kabla yake."

John 3:29

Viunganishi vya maneno:

Yohana Mbatizaji anaendelea kuongea.

Yeye aliye naye bibi harusi ndiye bwana harusi

Hapa bwana na "bibi" "arusi" ni mfano. Yesu ni kama "bwana arusi" na Yohana ni kama rafiki wa bwana arus." "bwana huoa bibi

Hii, tena, furaha yangu imetimilizwa

'' Hivyo tena ninafurahia sana" au nina furahia zaidi."

furaha yangu

hili neno "yangu" lina maanisha Yohana Mbatizaji , ndiye anayeongea.

Ni lazima aongezeke

anamaanisha bwana arusi, Yesu, ambaye ataendelea kuwa wa muhimu.

John 3:31

Yeye ajaye kutoka juu yu juu ya yote

Yohana anaongea kuhusu Yesu. "Yeye ajaye kutoka mbinguni ni wa muhimu zaidi yeyote.

Yeye aliye wa chini ni wa chini na huongea mambo ya chini

Yohana anajipinga mwenyewe dhidi ya Yesu. hamaanishi kuwa kwa kuwa alizaliwa duniani ni mwovu. Ana maanisha kuwa Yesu ni mkuu kuliko yeye kwa sababu Yesu alitoka mbinguni na Yohana alizaliwa hapa duniani. "Yeye aliyezaliwa hapa duniani ni kama mtu yeyote na na anaishi na anaongea kuhusu kilichotokea duniani."

hakuna mtu apokeaye ushuhuda wake

Yohana anaongea kwa kuonyesha neno katika hali ya kulikuza neno kwamba ni watu wachache walimwamini Yesu. "Watu wachache walimwamini."

Yeye apokeaye ushuhuda wake

Aliye ina maanisha mtu. " Mtu yeyote anayeamini kile ambacho Yesu alikisema."

amethibitisha

"kuthibitisha" au "inakubaliana"

John 3:34

Kiiunganishi cha Sentesi:

Yohana Mbatizaji anamaliza kuongea."

Kwa maana yeye ambaye Mungu amemtuma "

Huyu Yesu, ambaye Mungu amemtuma kumwakilisha."

kwa kuwa hatoi Roho kwa kipimo

" Kwa sababu yeye ndiye ambaye Mungu amempa nguvu zote za Roho wake."

Baba...Mwana

Hiki ni cheo kinachoelezea uhusiano wake kati ya Mungu na Yesu.

amepewa...katika mikono yake

Hii ina maanisha kuwekwa katika nguvu zake au kuotawala.

Yeye aaminiye

"Mtu aaminiye" au "mtu yeyote aaminiye."

ghadhabu ya Mungu inamkalia

Nomino dhaniwa "ghadhabu" linaweza kufasiriwa kama kitenzi "adhibu." "Mungu ataendelea kumwadhibu."

John 4

Yohana 04 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Yohana 4:4-38 ni habari moja inayozingatia mafundisho ya Yesu kama "maji yaliyo hai," anayewapa wote wanaomwamini uzima wa milele. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#believe)

Dhana maalum katika sura hii

"Ilikuwa ni lazima yeye apitie Samaria"

Kwa kawaida, Wayahudi wangeepuka kusafiri kupitia eneo la Samaria. Wasamaria walionekana kama watu wasiomcha Mungu kwa sababu walikuwa kizazi cha ufalme wa kaskazini mwa Israeli ambao walioana na wapagani. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#ungodly, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#kingdomofisrael and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

Mahali sahihi pa ibada

Mojawapo ya dhambi kubwa zaidi zilizofanywa na watu wa Samaria katika historia ni kwamba walianzisha hekalu la uongo katika wilaya yao ili kushindana na hekalu huko Yerusalemu. Huu ndio mlima mwanamke anayezungumzia katika Yohana 4:20. Wayahudi walisema kwa haki kwamba Waisraeli wote waabudu huko Yerusalemu kwa sababu ndipo ambapo Yehova aliishi. Yesu anaelezea kwamba mahali pa hekalu hapajalishi tena. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

Mavuno

Taswira ya kuvuna hutumiwa katika sura hii. Hii ni mfano ambayo inawakilisha watu kuwa na imani katika Yesu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith)

"Mwanamke Msamaria"

Mwanamke Msamaria labda ilitumika ili kuonyesha utofauti na hisia za Kiyahudi kumhusu Yesu. "Yesu mwenyewe alinena kwamba nabii hana heshima katika nchi yake" (Yohana 4:44). Kulikuwa na sababu nyingi ambazo Wayahudi wangeweza kumwona mwanamke huyu kama asiyeaminika. Alikuwa Msamaria, mzinzi, na mwanamke. Licha ya hii, alifanya kile alichohitaji Mungu. Alimwamini Yesu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#prophet, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#adultery and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#believe)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Katika roho na kweli"

Ibada ya kweli haielekezwi tena kwa mahali moja, lakini sasa imeelekezwa kwake Yesu. Mbali na hayo, ibada haifanywi tena kwa kupitia makuhani. Kila mtu anaweza kumwabudu Mungu mwenyewe kwa njia ya moja kwa moja. Kifungu hiki kinamaanisha kwamba ibada sahihi kwa Mungu inaweza sasa kufanywa bila kutoa sadaka ya kuchinjwa na inaweza kufanywa kikamilifu kwa sababu ya ufunuo mkubwa uliotolewa kwa mwanadamu. Kuna ufahamu zaidi wa ziada wa kifungu hiki. Inaweza kuwa bora kuyaacha maneno haya kwa hali ya kawaida kama iwezekanavyo katika tafsiri ili kutoondoa maana nyingine iliyopo. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#reveal)

<< | >>

John 4:1

Maelezo kwa Ujumla:

Huu ni sehemu nyingine ya simulizi ambayo inamuhusu Yesu na mwanake Msamalia. Mstari huu unatoa habari ya mwanzoni kwa ajili ya sehemu ya simulizi

Basi Yesu alipofahamu

Neno "sasa" limetumika hapa kuonyesha kusimama kidogo katika simulizi kuu. Hapa Yohana anaanza kuelezea sehemu mpya ya simulizi.

Yesu mwenyewe hakuwa anabatiza

Nomino hii mwenyewe inongeza msisitizo kwmba sio kwamba Yesu mwenyewe alikuwa akibatiza, bali wanafunzi wake.

John 4:4

eneo la

"sehemu ya ardhi" au "kipande cha ardhi"

John 4:6

Nipe maji

Hili ni ombi la upole, na sio amri.

John 4:9

Kisha mwanamke Msamalia akamwambia

Neno "akamwambia" linamaanisha Yesu.

Inawekanaje wewe uliye Muyahudi unaomba maji ya kunywa?

Hili neno linaonekana katika muundo wa swali kuonesha mshangao wa mwanamke kwa Yesu kuomba maji. "Siamini kama wewe uliye Muyahudi unamwomba mwanamke Msamalia maji!"

hamchangamani na

"hamchangamani na."

maji ya uzima

Yesu anatumia mfano "maji ya uzima" kumaanisha Roho Mtakatifu ambaye anafanya kazi ya kumbadilisha mtu na kuleta maisha mapya.

John 4:11

wewe si mkuu, je wewe ni mkuu kuliko baba yetu Yakobo... mifugo?

hili neno linaonekana katika muundo wa swali na kuonesha msisitizo, "wewe sio mkuu kama zaidi ya baba yetu... naYakobo... mifugo?

baba yetu yakobo

"babu yetu Yakobo"

alikunya maji ya kisima hiki

alikunywa maji yaliyoka katika kisima

John 4:13

atapata kiu tena

"atahitaji kunywa maji tena.""

maji nimpayo yatakuwa chemchemi ndani yake

Neno "chemchemi" ni fumbo kwa maji yatiayo uzima. "maji nitakayompa yatakua kama chemchemi ya maji ndani yake."

uzima wa milele

hapa "uzima" lina maanisha "uzima wa kiroho" ambao ni Mungu pekee anayeweza kutoa.

John 4:15

Bwana

katika mkitadha huu, mwanamke Msamalia anamwita Yesu "Bwana" ambayo ni neno la upole au unyenyekevu.

teka maji

"pata maji" au "vuta maji kutoka ndani ya kisima" kwa kutumia chombo na kamba

John 4:17

Umenena vyema... Katika hili umenena vyema

Yesu anarudia kauli hii kusisitiza kuwa anafahamu kuwa mwanamke anaongea ukweli.

John 4:19

Bwana

Katika mkitadha huu mwanamke Msamalia anamwelezea Yesu kama "Bwana," ambalo ni neno la heshima na upole.

Naona ya kuwa unabii

"Naelewa kuwa unabii."

mababa

Mababu wa zamani

John 4:21

niamini

Kumwamini mtu ni kukubali kuwa alichokisema ni kweli.

Ninyi mwaabudu msichokijua. Twaabudu kile tukijuacho

Yesu alimaanisha kuwa Mungu amajifunua na amri zake kwa Wayahudi, sio kwa Wasamalia. Kupitia maadiko Wayahudi wanajua Mungu ni nani kuliko Wasamalia.

Mtamwabudu Baba...kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi

Wokovu wa milele kutoka dhambini unatoka kwa Mungu Baba, ambaye ni Yaweh, Mungu wa Wayahudi.

Baba

Hiki ni cheo muhimu kwa Mungu.

Kwa sababu wokovu watoka kwa Wayahudi

Hii haimaanishi kuwa Wayahudi watawaokoa wengine kutoka dhambini. Ina maanisha kuwa Mungu amewachagua Wayahudi kama watu maalumu ambao watakaowambia watu wengine kuhusu wokovu wake. "kwa sababu watu wote watafahamu wakovu wa Mungu kwa sababu ya Wayahudi.

John 4:23

Kiunganishi cha Sentesi:

kuabudu ka

Ingawa, saa inakuja, na sasa ipo, ambapo waabudu wa kweli wata

"Ingawa, huu ni wakati sahihi kwa waabudu w kweli."

Baba

Hiki ni cheo muhimu cha Mungu.

kuabudu katika roho na kweli

"kumwabudu katika njia sahihi."

John 4:25

Ninafahamu kwamba Masihi...Kristo

Haya maneno mawili yana maanisha "mfalme aaliyeahidia na Mungu."

atatwambia kila kitu

Haya maneno "atawambia kila kitu" yanamaanisha mambo yote ambayo watu wanahitaji kujua. "atatwambia kila kitu tunachohitaji kufahamu."

John 4:27

Wakati huo wanafunzi wake wakarudi

"wakati Yesu alipokuwa akiyasema haya wanafunzi wake walirudi kutoka mjini."

nao walikuwa wakishangaa kwa nini alikuwa akiongea na mwanamke

lilikuwa ni jambo la nadra kwa Muyahudi kuongea na mwanamke asiye mfahamu.

John 4:28

Njoni mumwone mtu aliyeniambia kila kitu nilichotenda

Hii ni hali ya kusema jambo dogo kwa kulikuza. Mwanamke Msamalia anavutiwa na Yesu na kwamba anaamini kuwa Yesu anawelewa mambo yote. "Njooni mumwone mtu anaye fahamu mengi zaidi kunihusu, pamoja kwamba sijawahi kukutana naye!"

Yamkini akawa ndiye Kristo, inawezakana?

Mwanamke hana uhakika kuwa Yesu ni Kristo, kwa hiyo anauliza swali ambalo linahitaji jibu la '"hapana" lakini anauliza swali badala ya kuweka sentesi kwa sababu anataka watu wenyewe waamue wenyewe.

John 4:31

Wakati wa mchana

"Wakati mwananamke alipokuwa akienda mjini"

Wanafunzi walikuwa wakimuuliza

"wanafunzi walikuwa wakimwambia Yesu" au wanafunzi walikuwa wakimtia moyo"

Ninacho chakula ambacho hamkijui

Hapa Yesu haongelei "chakula" bali anawaandaa wanafunzi wake kwa ajili ya fundisho la kiroho.

Hakuna mtu ambaye amemlea kitu chochote

Wanafunzi wanafikiri kuwa anaongelea chakula cha kawaida.Wakaanza kuulizana wakitegemea mwitikio wa hapana. Hakika hakuna mtu aliye mletea chakula tulipokuwa mjini!"

John 4:34

chakula changu ni kufanya mapenzi yake aliyenituma na kutimiza kazi yake

"Chakula" hapa ni lugha ya picha inayowakilisha "kutii mapenzi ya Mugu." Kama vile ambavyo chakula kinavyo mtoshelea mwenye njaa, kutii mapenzi ya Mungu ndich kinachonitosheleza."

Je hamsemi

'Je hii sio miongoni mwa misemo yenu maarufu"

tazameni mashamba, kwa sababu yako tayari kwa mavuno

maneno haya mashamba na mazao yaliyo tayari yana lugha ya picha. Mashamba yanawakilisha watu wa mataifa. Na neno wako tayari linamaanisha utayari wa watu wa mataifu wa kupokea ujumbe wa Yesu kama vile mashamba yalivyo tayari kwa kuvunwa. "tazameni hawa watu wa mataifa!wako tayari kupokea ujumbe wangu, kama vile mazao katika mashamba yalivyo tayari kwa ajili ya kuvunwa."

Yeye avunaye anapokea posho na hukusanya matunda kwa uzima wa milele

Yesu anaonyesha kuwa kuna tuzo kwa wale "wanaofanya kazi katika mashamba" na kuwashirikisha ujumbe wake wengine. Na yule atakaye pokea ujumbe atapokea pia uzima wa milele ambao Mungu anawapa watu.

John 4:37

Kiunganishi cha Sentesi:

Yesu anaendelea kuongea na wanafunzi wake.

Mmoja hupanda na mwingine huvuna

Maneno "kupanda" na kuvuna ni maneno ya lugha ya picha. Yeye anayepanda anashirikisha ujumbe wa Yesu. Yeye anayevuna anawasaidia watu kupokea ujumbe wa Yesu." Mtu mmoja hupanda mbegu, na mwingine huvuna mazao."

ninyi wenyewe mmeingia katika kazi zao

ninyi wenyewe hutia msisitizo kwa neno "wewe" tafsiri hili katika lugha yako katika namna ya kumsisitiza mtu.

John 4:39

muamini katika yeye

"Kuamini katika" maana yake ni "kuamini katika" huyo mtu. Hapa pia ina maanisha kuwa waliamini kuwa alikuwa Mwana wa Mungu.

ameniambia mambo yangu yote niliyofanya

hili ni hali ya kuelezea jambo dogo katika hali kulifanya jambo kuwa kubwa zaidi ya lilivyo. Mwanamke alivutiwa sana na Yesu na akahisi kuwa lazima akuwa anajua kila kitu kumuhusu yeye. "Ameniambia mambo mengi kuhusu maisha yangu."

John 4:41

neno lake

"Neno" hapa lina sisimama kwa kumaanisha ujumbe ambao Yesu alihubiri. "ujumbe wake"

ulimwengu

ulimwengu hapa unasimama kwa kumaanisha watu wote wanaoishi duniani. "Watu wote wanaoishi duniani."

John 4:43

Maelezo kwa Ujumla:

hii ni sehemu ya simulizi ambayo Yesu anatelemka kwenda Galilaya na anamponya kijana.Mstari 44 inatupa habari kuhusu kitu ambacho Yesu alikuwa amekisema mwanzoni.

Kwa kuwa Yesu mwenyewe alitangaza

yeye mwenyewe limeongezwa kwa kutia msisitizo kwamba Yesu alikuwa ametangaza" au alisema haya.. Unaweza kuliweka katika lugha kwa jinsi ya kutia msisitizo kwa mtu.

nabii hana heshima katika nchi yake

Watu haonyeshi heshima au kumuhesimu nabii wa nchi ya kwao" au "nabii haheshimiwi na watu wa jamii yake."

kwenye sikukuu

sikukuu hapa ni Pasaka.

John 4:46

Sasa

Neno hili linaonyesha ukomo wa masimulizi na kuhamia sehemu nyingine ya simulizi. kama katika lugha yako kuna jinsi ya kuweka hili unaweza kuweka.

afisa

mtu ambaye yuko katika huduma ya mfalme

yuko katika hali ya kufa

"kuwa katika hali kufa."

John 4:48

ninyi hamwezi kuamini hadi mwone ishara na maajabu

Msipo...hamwe kuamini" ni mashaka hasi. Katika lugha nyingine hili linatafsiriwa katika mtazamo chanya. "Mtaamini tu pale mtakapoona miujiza."

kuliamini neno

Hapa "neno" lina maanisha ujumbe ambao Yesu alioutoa. "amini ujumbe."

John 4:51

Wakati

hili neno limetumika kuonesha matukio mawili ambayo yanatokea kwa wakati mmoja. Afisa alipokuwa akienda nyumani, wafanya kazi wake wakimpokea njiani.

John 4:53

Kwa hiyo akaamini yeye na nyumba yake yote

yeye mwenyewe imetumika kusistiza neno "yeye" kama katika lugha yako una namna ya kusema unaweza kufikiri namna ya kutumia.

Ishara

Miujiza inaweza kuitwa "ishara" kwa sababu yametumika kama kiilelezo cha ushahidi kuwa Mungu ni mwenye nguvu zaidi na aliye na mamlaka juu ya dunia.

John 5

Yohana 05 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Baraza

Wayahudi wengi waliamini kwamba baraza hizi zilikuwa na uwezo wa kuponya. Hii ilifanyika wakati maji "yalichochewa." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

"Ufufuo wa hukumu"

Haya ni marejeo ya wakati baada ya kifo ambapo watu wote watahukumiwa. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#death and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#judge)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Mwana, Mwana wa Mungu

Yesu anajiita mwenyewe kama "Mwana," "Mwana wa Binadamu" na "Mwana wa Mungu." Lugha zingine haziwezi kuruhusu mtu kujielezea katika 'mtu wa tatu.' (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sonofman and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sonofgod)

"Ameshuhudia juu yangu"

Yesu anazungumza juu ya Agano la Kale kushuhudia kumhusu yeye. Agano la Kale linatoa unabii mwingi kuhusu Masihi ambayo yalielezea kuhusu Yesu kabla ya kuja kwake duniani. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#prophet and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#christ)

<< | >>

John 5:1

Maneno kwa Ujumla:

hili ni tukio linalofuata katika simulizi,ambalo Yesu anapanda kwenda Yerusalemu na anamponya mtu.Mistari hii inatoa mambo ya nyuma kuhusu mwanzoni mwa simulizi.

Baada ya hili

ina maanisha baada Yesu kumponya mwana wa afisa. ona namna ambavo unaweza kufasiri hili.

kulikuwa na sikukuu ya Wayahudi

"Wayahudi walikuwa wakisherehekea sikukuu"

alipanda kwenda Yerusalemu

Yerusalemu iko juu ya kilima. Mabarabara ya Yerusalemu yalipanda juu na kutelemka katika vilima vidogo . Kama lugha yako ina neno tofauti kwa kupanda juu ya kilima kuliko kuliko kutembea katika tambarare unaweza kuitumia hapa.

dimbwi

hili lilikuwa ni shimo chini ambalo watu walijaza maji. Wakati mwingine walilizungushia kwa vigae na mawe.

Bethzatha

"Bethzatha" maana yake ni nyumba ya huruma.

matao

muundo ulioezekwa angalau pasipo kuwa ukuta mwingine katika jengo.

Idadi kubwa ya watu

"watu wengi"

John 5:5

Maelezo kwa Ujumla:

Mstari wa 5 unatambulisha mtu amelala pembeni mwa dimbwi la simulizi.

kulikuwa

"Kulikuwa kwenye dimbwi la Bethzatha"

amekuwa hawezi

"amepoza"

miaka thelathini na minane

miaka minane - miaka 38

akatambua

"alifahamu" au "alipata kuelewa"

akamwambia

"Y esu akamwambia yule mtu aliye poza"

John 5:7

Bwana, sina

hapa neno "Bwana" ni namna ya kumkabili mtu wa upole. "Bwana, hakuna mtu"

wakati maji yanapotibuliwa

Hii linaweza kufasiriwa katika muundo tendaji. "wakati malaika hutibua maji"

ndani ya dimbwi

hili lilikuwa ni shimo katika chini ambalo watu walijaza maji. wakati mwingine walilizungushia kwa vigae na mawe.

mwingine huenda mbele yangu

watu walishuka kwa hatua kadhaa kuingia ndani ya maji. "mtu mwingine mara zote huingia ndani ya maji kabla yangu.

Inuka

"simama!"

chukua kitanda chako na uende

"Chukua godor lako la kulalia, na utembee!"

John 5:9

mtu aliponywa

"mtu alikuwa na afya tena"

Sasa

Neno "sasa" limetumika hapa kwa ajili ya Yohana kutoa historia ya nyuma kwamba tukio hili linatukia siku ya Sabato.

John 5:10

Basi

hili neno linaonyesha tukio ambalo lilitokea kwa sababu ya kitu fulani kutokea. Katika hili Yesu alikuwa

Yeye aliye nifanya kuwa mzima

"Mtu aliye nifanya mzima."

John 5:12

Wakamuuliza

"Viongozi wa Kiyahudi wakamuuliza mtu aliyeponywa"

John 5:14

Yesu akampata

"Yesu alimpata mtu aliye mponya

Tazama

"Tazama" au "Sikiliza" au "Tilia manani kile ninachokueleza"

John 5:16

Basi

'Basi" linamwonesha Yohana anatoa kwa ufupi kuhusu tabia za viongozi wa Kiyahudi kwa Yesu.

kazi

Hii ina maanisha shughli au kitu chochote kinachofanywa kuwatumikia watu.

akijifanya yeye kuwa sawa na Mungu

"sema kwamba alikuwa sawa na Mungu"au kusema kwamba alikuwa na mamlaka makuu kama Mungu"

Baba yangu

Hiki ni cheo muhimu kwa Mungu

John 5:19

Kiunganishi cha sentesi:

Yesu anaendelea kuongea na viongozi wa Wayahudi.

Amini, amini

Tafsiri hii kama ulivyo tafsiri 1:49; 1:51

mtashangazwa

"mtashangazwa" au mtasitushwa"

chochote anachofanya Baba, Mwana anayafanya haya mambo pia. Kwa Baba anampenda Mwana

Yesu, kama Mwana wa Mungu, alifuata na kutii uongozi wa Baba yake chini ya nchi kwa sababu Yesu alijua Baba anampenda.

Mwana...Baba

Hivi ni vyeo muhimu ambavyo zinaelezea uhusiano kati ya Yesu na Mungu.

penda

aina hii ya upendo unatoka utokao kwa Mungu unajali mazuri ya wengine, hata kama haina faida yake. Mungu mwenyew ni upendo na chanzo cha upendo wa kweli.

John 5:21

Kama vile Baba afufuavyo wafu na kuwapa uzima...Mwana pia humpa uzima kwa yeyote apendaye

Neno "kwa" ni linganifu Mwan wa Mungu (Mungu Mwana) anatoa maisha kama Mungu Baba anavyotoa uzima.

Baba...Mwana

Hivi ni vyeo ambavyo vinaelezea uhusiano kati ya Mungu na Yesu.

uzima

ina maanisha "uzima wa kiroho."

Kwa kuwa Mwana Baba hamhukumu mtu yeyote, bali amempa Mwana uwezo wote wa kuhukumu.

Neno "kwa" linaonesha ulinganifu. Mwana wa Mungu ndiye anayehukumu kwa niaba ya Mungu Baba.

mheshimu Mwana kama ...Baba. Yeye amuheshimu Mwana hamheshimu Baba

Mungu Mwana ni lazima aheshimiwe na kuabudiwa kama vile ambavyo Mungu Baba. Kama tukishindwa kumuheshimu, pia tunashindwa kumuheshimu Mungu Baba.

John 5:24

Amini, amini

Tafsiri hii kama ulivyo tafsiri

hatahukumiwa bali

"atahukumiwa kuwa hana hatia na"

John 5:25

Amini, amini

Tafsiri hii kama ulivyotafsiri mahali pengine pa "amini, amini."

wafu wataisikia sauti yangu,Mwana wa Mungu, na wao waisikiao watakuwa hai

Sauti ya Yesu , Mwana wa Mungu, itawafufua wafu kutoka makaburini.

Mwana wa Mungu

Hiki ni cheo muhimu kwa Yesu.

John 5:26

Kama vile Baba alivyo na uzima ndani yake, vivyo hivyo amempa Mwana ili awe na uzima ndani yake

Neno "kwa" linaonyesha ulinganifu. Mwana wa Mungu ana uzima sawa kama aliona nao Baba.

Baba...Mwana wa Adamu

Hivi ni vyeo muhimu vinavyoelezea ushirika kati ya Mungu na Yesu.

uzima

hii ina maanisha uzima wa kiroho

Baba amempa Mwana Mwana uwezo kufanya hukumu

Mwana wa Mungu ana mamlaka ya Mungu Baba kuhukumu.

John 5:28

sikia sauti yake

"sikia sauti ya Mwana wa Adamu"

John 5:30

kutofanya chochote kutoka

Tafsiri hii kama ulivyo tafsiri 5:19

mapenzi ya aliyenituma mimi

Neno "aliye" lina maanisha Mungu Baba

John 5:33

ushuhuda ninao pokea sio wa mwanadamu

"Sihitaji ushuhuda wa watu"

okolewa

Hii ina maanisha "kuokolewa" ni katika maana ya kiroho. Kama mtu amekwisha "akolewa" ina maanishakwambaMungu amekwisha msamehe na kumuokoa kutoka katika adhabu ya Jehanamu kwa ajili ya dhambi zake.

Yohana alikuwa ni taa iliyokuwa ikiwaka na kung'ara

Yohana anonesha utakatifu wa Mungu kama vile ambavyo taa itoavyo mwanga.

John 5:36

kazi alizonipa Baba kuzitimiliza ...zinashuhudia...kuwa Baba amenituma

Mungu Baba amemtuma Mungu Mwana, Yesu, Mwana wa Mungu, duniani. Yesu anatimiza kile ambacho Baba amempa kufanya.

Baba

Cheo muhimu kwa Mungu

hamana neno lake...ndani yenu, kwa sababu hamumwamini yeye aliyemtuma

"Hamuamini katika yeye aliyetumwa. Hivi ndivyo ninavyofahamu kuwa hamna neno lake ndani yenu." Kumjua Mungu wa kwelikatika Yesu, Mwana wa Mungu, ambaye Baba amemtuma. Maneno "Baba" na "Mwana" lazima yatafsiriwe katika utambulisho ambaye ni lazima tuamini.

likikaa ndani yenu

"kukaa pamoja nanyi

John 5:39

ndani yao mna uzima wa milele

"mtapata uzima wa milele kama mtasoma maandiko" au "maandiko yatakwambia namna mtakavyo pata uzima wa milele."

Ili mpate uzima

"uzima" hapa ina maanisha "uzima wa milele."

John 5:41

pokea

"pokea"

hamna upendo wa Mungu ndani yenu

Hii ina maanisha 1)"kweli kabisa hamumpendi Mungu" au 2)"kweli hamjapokea upendo wa Mungu."

John 5:43

katika jina la Baba yangu

Hapa neno "jina" lina maanisha mamlaka na nguvu za Baba.

Baba

Cheo muhimu kwa Mungu.

pokea

"pokea"

mtawezaje kuamini, ninyi ambao hupokea ...Mungu?

"Hakuna namna mnaweza kuamini kwa sababu mnapokea sifa... Mungu!"

amini

hii ina maanisha kuamini katika Yesu.

Nimekuja kwa jina la Baba yangu...kutoka kwa Mungu pekee

Yesu amekuja duniani kwa jina la Mungu Baba, Mungu pekee.

John 5:45

Yupo mwingine ambaye anawashitaki

Mungu alitoa sheria, ili kwamba mahitaji ya agano, kwa Israeli kupitia Musa. Hiki ndicho Wayahudi walimaanisha walipokuwa wakisema, "Musa alitupa sheria."Lakini kwa Waisraeliambao hawakutii sheria, Yesu alimaanisha kuwa Musa angewa shitakikwa kutokutii. Lakini "Musa" anasimama hapa kwa niaba ya sheria yenyewe.

matumaini yenu

"ujasiri wenu'

kama hamyaamini maandiko yake, mtawezaje kuamini maneno yangu?

"Hamuamini maandiko , hivyo hamtaamini maneno yangu!"

maneno yangu?

"Ninachosema?"

John 6

Yohana 06 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

"Wamfanye mfalme"

Ingawa si wasomi wote wanakubaliana juu ya sababu halisi ambayo Yesu hakutaka kuwa mfalme, kwa ujumla walikubaliana kuwa watu hawakuwa na nia nzuri ya kumfanya awe mfalme. Walitaka awe mfalme kwa sababu aliwapa chakula. Walikosa kutambua ukweli kwamba amekwisha kuwa mfalme wa wafalme. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

Mkate

Yesu anatumia taswira ya mkate katika sura hii. Umuhimu wa mkate asili yake ni utoaji wa kila siku ambao Mungu alitoa kwa Israeli jangwani kwa miaka 40 na matukio ya Pasaka. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#passover)

Eating the flesh and drinking the blood

When Jesus said, "Unless you eat the flesh of the Son of Man and drink his blood, you will not have life in yourselves," he knew that before he died he would tell his followers to do this by eating bread and drinking wine. In the event this chapter describes, he expected that his hearers would understand that he was using a metaphor but would not understand what the metaphor referred to. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#flesh and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#blood)

Mimi ndimi

Yohana anatumia maneno haya mara saba katika injili yake. Ni maneno sawa yanayotumiwa na Mungu, alipojidhihirisha pamoja na jina lake Yahweh katika kichaka kilichokuwa kinawaka. Jina "Yahweh" linaweza kutafsiriwa kama Mimi ndimi."

Mfano muhimu za usemi katika sura hii

"Ananipa ... huja kwangu"

Maneno haya hutumiwa kumaanisha kwamba wengi "wataamini Yesu." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

"Kula mwili wangu na kunywa damu yangu"

Hii inapaswa kuonekana wazi kama mfano. Ni marejeo ya mazoezi yaliyoanzishwa wakati wa chakula cha mwisho cha Yesu wakati Yesu alitumia mkate na divai kuwakilisha mwili wake na damu. Hii ni kumbukumbu ya kifo cha Yesu kwa dhambi. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#flesh, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#blood and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Mawazo kwenye mabano

Mara kadhaa katika kifungu hiki, Yohana anaandika maelezo mengine ili msomaji afahamu vizuri habari. Maelezo haya yanalenga kumpa msomaji ujuzi wa ziada bila kudakiza uandishi. Maneno haya yanawekwa ndani ya mabano.

"Mwana wa Binadamu, Mwana"

Yesu anajiita mwenyewe kama "Mwana wa Binadamu." Lugha zingine haziwezi kuruhusu mtu kujitaja mwenyewe kama 'mtu wa tatu.'

<< | >>

John 6:1

Maelezo ya Jumla:

Hii ni sehemu ya pili ya simulizi. Mkutano ulikuwa umemfuata Yesu juu ya mlima. Mistari hii inazungumzia mahali ambapo simulizi inaanzia.

Baada ya mambo haya

Neno " haya mambo" ina maanisha matukio katika. "wakati mwingine baadaye."

Yesu akaenda zake

"Yesu akaenda mahali" au "Yesu kasafiri"

John 6:4

Maelezo kwa UJumla:

kitendo katika simulizi kinaanza msitari wa 5.

(Pasaka, sikukuu ya Wayahudi ilikuwa karibu.)

Yohana kwa ufupi anaacha kuongea kuhusu matukio katika simulizi ili kwamba alete hisotia ya nyuma kuhusu lini tukio lilitokea.

(Basi Yesu alisema maneno haya ili kumjaribu Filipo, kwa sababu yeye mwenyewe alifahamu atakachokifanya.)

kwa ufupi Yohana anaacha kuongea kuhusu matukio katika simulizi ili kwamba afafanue kwa niniYesu alimuuliza Filipo mahali pa kunua mkate.

Kwa sababu yeye mwenyewe alifahamu

Neno "mwenyewe" hapa linaweka wazi kwamba neno "yeye" lina maanisha Yesu.Yesu alifahamu nini angefanya.

John 6:7

ya thamani ya dinari

" Mikate ambayo inagharimu mshahara wa siku mia mbili." Dinari ni wingi wa "dinari nyingi."

mikate ya shayili

mkate mdogo wa mvilingo uliotengenezwa kwa nafaka ya kawaida.

Hii itafaa nini kwa watu wengi?

hii"silesi chacheya mikate na samaki haitoshikulisha watu wengi."

John 6:10

kaa chini

au "kaa chini" tegemea na desturi yako

(Basi kulikuwa na nyasi nyingi katika sehemu ile.)

Hii ilikuwa ni sehemu nzuri kabisa kwa ajili ya watu kukaa.

watu... wanaume... watu

Mkutano

elfu tano kwa idadi

wakati mkutano pengine ulijumuisha wanawake na watoto.

akashukuru

Yesu aliomba kwa Mungu Baba na kumshukuru kwa ajili ya mkate na samaki.

aliwagawia

Yesu aliivunja mikate na samaki akawapitishia wanafunzi wake. Kisha wanafunzi wakawapitishia watu mikate na samaki.

John 6:13

Maelezo ya Jumla:

Yesu anajitoa katika mkutano. Hii ni sehemu ya mwisho ya simulizi kuhusuYesu kuwalisha mkutano juu ya mlima.

wakakusanyika

"Wanfunzi wakakusanya"

wakaacha

chakula ambacho hakuna mtu aliye amekila

ishara hii

Yesu anawalisha watu 5000kwa mikate mitani ya shairi na samaki wawili.

John 6:16

Kiunganishi cha Maneno:

ili ni tukio linalofuata katika simulizi;wanafunzi wa Yesu wanaenda ziwani.

(wakati giza lilikuwa limeingia, na Yesu alikuwa bado hajaenda kwa wanafunzi.)

Tumia lugha yako jinsi ya kuonesha hii ni habari ya nyuma ya habari.

John 6:19

wanafunzi wake wakuwa wamepiga makasia

kwa kawaida mitumbwi ilikuwa na watuwawili, au sita watu waliopiga makasia kwa pamoja. Mila yako inaweza ikawa na namna nyingine ya kusababisha mtumbwikukatisha katika maji mengi .

kama makasia ishirini na matanoau thelathini

tano au makasia sita "kama kilometa tano au sita." kasia ni kama makasia, mita 185.

John 6:22

bahari

Bahari ya Galilaya

(Ingawa, palikuwa... Bwana aliposhukuru)

tumia lugha yako kuonesha kuwa hii ni habari ya nyuma.

mitumbwi iliyokuja kutoka Tiberia

siku iliyofuata baada ya Yesu kuwalisha watu, baadhi ya mitumbwi kutoka Tiberia ilikuja na watu ili wamwone Yesu.Ingawa, Yesu na wanafunzi wake walikuwa wametoka usiku mmoja kabla.

John 6:24

Maelezo ya Jumla:

mkutano unaanza kumuuliza Yesu maswali

John 6:26

Amini, amini

tafsiri hili kama ulivyo tafsiri mengine kama haya maneno.

uzima wa milele ambao Mwana wa Adamu atawapa ninyi, Mungu Baba ametia muhuri juu yake

Baba amfanya uthibitisho wake kwa Yesu, Mwana wa Adamu na Mwanawa Mungu, kutoa uzima wa milele kwa wale wanao amini katika yeye. Baba na Mwana wamekwisha timiza msamaha wa milele na uzima.

Mwana wa Adamu, Mungu Baba

Hivi ni vyeo muhimu ambavyo zinaelezea uhusiano kati Mungu na Yesu.

ametia muhuri juu yake

"ametia muhuri" juu ya kitu maana yake kuweka alama juu yake kuonesha ina milikiwa na.Hii ina maana kuwa Mwana anatokana na Baba.

John 6:30

mababa

"mababa wa zamani"

mbingu

Ina maanisha sehemu ambayo Mungu huishi

John 6:32

Amini, amini

Tafsiri hili kama ulivyo tafsiri maneno kama haya.

Baba yangu ndiye awapaye mkate wa kweli kutoka mbinguni

Baba anatupa "mkate wa kweli" kutoka mbinguni, Mwanae Yesu. Pamoja Baba na Mwana pamoja na Roho Mtakatifu wanawapa watu maisha ya kimwili, kiroho na maisha ya milele.

Baba yangu

Hiki ni cheo muhimu kwa Mungu.

mkate wa kweli

Yesu anajilinganisha na mkate. Kama vile mkate uliyo muhimu kwa ajili ya maisha yetu ya mwili, Yesu ni wa muhimu kwa ajili ya maisha yetu ya kiroho.

uzima

hili lina maanisha uzima wa kiroho.

John 6:35

Mimi ni mkate wa uzima

Yesu anajifananisha na mkate. Kama vile mkate ulivyo muhimu kwa maisha yetu ya mwili, Yesu ni wa muhimu kwa maisha yetu ya kiroho.

aaminiye katika

Hii ina maanisha kuaminia kuwa Yesu ni Mwan wa Mungu, kumtegemea kama mwokozi, na kuishi katika namna ambayo ina mpendeza.

Wale wote anipaye Baba watakuja kwangu

Mungu Baba na Mungu Mwana ni washirika katwa milele kwa wale wanao mwamini Yesu, Mwana wa Mungu.

Baba

Cheo muhimu kwa Mungu.

Yeye ajaye kwangu sitamtupa kamwe nje

"Nitamtunza kila mmoja ambaye ajaye kwangu.

John 6:38

Kiunganishi cha Maneno:

Yesu anaendelea kuongea na mkutano

yeye aliyenituma

"Baba yangu, aliyenituma mimi"

nisimpoteze hata mmoja

"Niwatunze wote"

mapenzi ya Baba yangu...kila amtazamaye

Yesu anafafanua kwamba Mpango wa Baba unatoauzima wa milele kwa walew wanaoamini " Mwana,"Mwana wa Mungu, Yesu Kristo atakaye fufua na kutukuza miili ya wote wanao amini.

Mwana na kuamini katika yeye awe na uzima wa milele

Yesu anafafanua kwamba mpango wa Mung unaleta uzima wa milele kwa wale wote wanao mwanini "Mwana," Mwana wa Mungu, Yesu Kristo, ambaye atakaye wafufua na kutukuza miili ya wale wanaoamini.

John 6:41

Kiunganishi cha Maneno:

Viongozi wa Wayahudi wanaingilia kati wakata Yesu anaongea na mkutano.

nung'unika

Kuongea katika hali ya kutokuwa na furaha

Mimi mkate wa uzima

Tafsiri hii kama ulivyotafsiri 6:35

John 6:43

kiunganishi cha maneno:

Yesu anaendela kuongea na mkutano na sasa anaongea na viongozi wa Wayahudi.

kuvuta

hii inaweza kufasiriwa 1) "kuvuta" 2)"kuvutia"

imeandikwa katika manabii

"Manabii waliandika"

Kila aliyekwisha sikia na kujifunza kwa Baba huja kwangu

Wayahudi walifikiri Yesu alikuwa mwana wa Yusufu" lakini ni Mwana wa Mungu kwa sababu Baba yake ni Mungu Baba , sio Yusufu. Wale wote ambao kweli wanajifunza kwa Mungu Baba wanaamini katika Yesu, Mungu Mwana.

Baba

Cheo muhimu kwa Mungu.

John 6:46

kinganishi cha maneno

Yesu anaendelea kuongea na mkutano na viongozi wa Wayahudi.

Amini, amini

Tafsiri hii kama ulivyo tafsiri maneno mengine ya namna hii.

hakuna mtua yeyote aliyemwona, isipokuwa yeye aliyetoka kwa Mungu

Ingawa hakuna mwadamu aishie katika dunia amemwona Mungu Baba, Yesu, Mwana wa Mungu, amemwona Baba.

Baba

Cheo muhimu kwa mungu.

yeye aaminiye ana uzima wa milele

"uzima wa milele" umeunganishwa katika Yesu, Mwana wa Mungu.

John 6:48

Mimi ni mkate wa uzima

Tafsiri hii kama ulivyotafsiri maneno yanayofanana na haya.

mababa

"mababa wa zamani"

kufa

hii ina maanisha kifo cha kimwili.

John 6:50

Huu ni mkate

tazama notisi 6:35

hakuna kufa

"ishi milele." hapa neno "kufa" lina maanisha kifo cha kiroho.

mkate wa uzima

Hii ina maanisha" mkate ambao una sababisha watu kuishi"

John 6:52

Kiunganishi cha maneno

Baadhi ya Wayahudi waliopo wanaanza kubishana wenyewe na Yesu anajibu kwa swali lao.

Amini, amini

tafsiri hili kama ulivyo tafsiri maneno mengine ya namma hii.

kula mwili wa Mwana Adamu na kunywa damu yake

Kumpokea Mwana wa Adamukwa imani ni sawa kupokea chakula na kinywaji.

John 6:54

Kiunganishi cha Sentesi:

Yesu anaendelea kuongea kwa wote wanao msikiliza.

chakula cha kweli... kinywaji cha kweli

Kumpokea Yesu kwa imani kunaleta uzima wa milele kama vile ambavyo chakula na kinywaji vinavyoawilisha mwili.

John 6:57

Baba mwenye uzima

Hii inaweza 1) "Baba atoaye uzima" au "Baba aishie," kama watu au wanyama wanavyoishi, kinyume cha "kifo"

Baba

hiki ni cheo muhimu kwa Mungu.

Baba mwenye uzima alinituma...kwa sababu ya Baba...yeye anilaye...ata...ishi kwa sababu ya

Yesu alitumwa na Baba, na anaishi kama mwanadamu kwa sababu ya Mungu Baba. Kama Mungu Mwana alivyotumwa na Mungu Baba, Yesu ni chanzo cha uzima wa milele.

mababa

"mababa wa zamani"

Yesu aliyasema mambo haya ndani ya Sinagogi... huku Kaperanaumu

hii ni babari ya nyuma kuhusu wakati tukio hili lilipotukia.

John 6:60

ni nani awezaye kulipokea?

"hakuna mtu anaweza kulipokea." au "halipokeleki."

Je hili lina kukwaza?

"Nin shangazwa kwamba hili lina wakwaza!"

linakukwaza wewe

"linakusababisha kukata tamaa kwa imani yako"

John 6:62

Basi ni vipi kama mkimwona Mwana wa Adamu akishuka kutokakule aliokuwa kabla?

"Labda mtaamini ujumbe wangu kama mkiniona, yeye aliye kuja kutoka mbinguni, akishuka kule nilikokuwa kabla!"

faida

Hii ina maanisha kusababisha vitu vizuri kutokea.

maneno

"Ujumbe" Pengine maana: 1) maneno yake ndani au 2) kila kitu anachofundisha.

maneno niliyokuambia wewe

"Nilichowambia"

roho

Maana zinazo wezekana ni 1)Roho Mtakatifu au2) vitu vya kiroho.

ni roho, na ni uzimaa

maana dhaniwa 1)"karibia Roho na uzima wa milele" au "kutoka kwa Roho na inatoa uzima wa milele" au 3)" ni kuhusuvitu vya kiroho na uzima."

John 6:64

hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amepewa na Baba

Mwana wa Mungu, amepewa na Baba. Mungu Baba na Mungu Mwana kwa pamoja ni njia katika wokovu msamaha wa milele. Yeyote atakaye kuamini ni lazima aje kwa Mungu kwa kupitia Baba na Mwana.

njoo kwangu

"nifuate mimi"

Baba

hiki ni cheo muhimu kwa Mungu

John 6:66

wanafunzi wake

"wanafunzi wake" hapa ina maanisha jumuisho ambao walimfuata Yesu.

kumi na wawili

Hili kundi maalumu ya wanaume 12 walio mfuata Yesu kwa huduma yake yote. Hii inaweza kufasiriwa "wafuasi kumi na wawili."

John 6:70

Je mimi sikuwachagua, ninyi kumi na wawili, na mmja wenu ni shetani?

"mwenyewe niliwachagua wote, lakini mmoja wenu ni mtumishi wa shetani."

John 7

Yohana 07 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

This whole chapter concerns the concept of believing Jesus to be the Messiah. Some people believed this to be true while others rejected it. Some were willing to recognize his power and even the possibility that he was a prophet, but most were unwilling to believe that he was the Messiah. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#christ and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#prophet)

Labda watafsiri watapenda kuandika alama katika mstari wa 53 kumwelezea msomaji kwa nini wamechagua kutafsiri au kutotafsiri mistari 7:53-8:11.

Dhana maalum katika sura hii

"Wakati wangu haujafika"

Kifungu hiki na "saa yake haujafika" hutumiwa katika sura hii kuonyesha kwamba Yesu alikuwa na uwezo juu ya vitu vilikuwa vinatoweka maishani mwake.

"Maji yaliyo hai"

Hii ni mfano muhimu inayotumiwa katika Agano Jipya. Ni mfano. Kwa sababu mfano huu unatolewa katika mazingira ya jangwa, labda inaonyesha kuwa Yesu anaweza kutoa chakula cha kudumisha maisha. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

Tamathali muhimu za usemi katika sura hii

Unabii

Yesu anatoa unabii juu ya maisha yake bila kutoa habari yote katika Yohana 7:33-34.

Kinaya

Nikodemo anawaelezea Mafarisayo wengine kwamba Sheria inamlazimisha asikie mtu moja kwa moja kabla ya kutoa hukumu juu yake. Mafarisayo kwa upande wao walifanya hukumu juu ya Yesu bila kuzungumza na Yesu.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Hawakumwamini"

Ndugu za Yesu hawakuamini kwamba Yesu alikuwa Masihi. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#believe)

"Wayahudi"

Neno hili linatumika kwa njia mbili tofauti katika kifungu hiki. Linatumika hasa kwa kutaja upinzani wa viongozi wa Kiyahudi waliokuwa wakijaribu kumwua (Yohana 7:1). Pia hutumiwa kwa kutaja watu wa Yudea kwa ujumla ambao walikuwa na maoni mazuri ya Yesu (Yohana 7:13). Mtafsiri anaweza kutumia maneno "viongozi wa Kiyahudi" na "watu wa Kiyahudi" au "Wayahudi (viongozi)" na "Wayahudi (kwa ujumla)."

<< | >>

John 7:1

Na baada ya mambo haya

"Na baada ya kumaliza kuongea pamoja na wanafunzi"

Safiri

"tembea"

John 7:3

ndugu

Hili linaelekeza kwa ndugu zake halisi, wana wa Mariamu na Yusufu.

Ulimwengu

"Watu wote" au "kila mmoja"

John 7:5

kaka zake

kaka zake wadogo

Wakati wangu bado haujafika

Yesu anamaanisha kuwa wakati muafaka bado haujafika kwa ajili ya huduma yake

John 7:8

Hawa

wingi

John 7:10

Naye vile vile alienda

Yerusalemu ilikuwa upande wa juu kutoka pale walipokuwa

Siyo kwa wazi bali kwa siri

Mafungu haya mawili yana maanisha jambo moja, iliyorudiwa kwa kuweka mkazo. Lugha zingine huweka mkazo kwa njia tofauti.

John 7:12

Hofu

Hili huchukuliwa katika hisia zisizokuwa za furaha wakati ambapo kuna utisho wa kuumizwa kwake au wengine.

John 7:14

Kwa jinsi gsni mtu huyu anajua mengi hivi?

"Haiwezekani akajua mengi juu ya maandiko."

Ni yeye aliyenituma

Neno "yeye" linamhusu Mungu Baba.

John 7:17

Lakini yeyete atafutaye utukufu wake aliyenituma, mtu huyo ni wa kweli na ndani yake hakuna kutokutenda haki.

"lakini ninafanya mambo ili kwamba wengine wapate kumheshimu yeye aliyenituma, nami ni yule asemaye kweli. Sidanganyi kamwe."

John 7:19

Musa hakuwapa ninyi sheria?

"Ni Musa aliyewapa ninyi sheria."

Kwa nini mnataka kuniua?

"Mnatafuta kuniua."

Una pepo

"Wewe ni kichaa."

Nani anataka kukuua?

"Hakuna yeyote anayetaka kukuua."

John 7:21

Kazi moja

"Muujiza mmoja" au "ishara moja"

(Siyo kwamba inatoka kwa Musa, lakini inatoka kwa mababa)

Hapa mwandishi anatoa maelezo ya nyongeza.

John 7:23

Kwa nini mnanikasirikia mimi kwa sababu nimemfanya mtu kuwa mzima katika siku ya Sabato"

"Hamkupaswa kunikasirikia kwa sababu nimemfanya mtu kuwa mzima siku ya Sabato."

John 7:25

Siye huyu wanayemtafuta kumwua?

"Huyu ni Yesu wanayemtafuta kumwua."

John 7:28

Ninyi nyote mnanijua na mnajua ninakotoka

"Ninyi" iko katika wingi.

Ni kweli

"Ni shahidi wa kweli."

John 7:30

Kristo atakapokuja, atafanya ishara zaidi ya hizi anazofanya mtu huyu?

"Kristo atakapokuja hataweza kufanya ishara zaidi ya hizi ambazo mtu huyu amefanya."

Ishara

"Hii inamaanisha miujiza inayothibitisha kuwa yeye ni Kristo."

John 7:33

Yeye aliyenituma

Mungu Baba

John 7:35

Mtawanyiko

Wayahudi sehemu mbali mbali katika ulimwengu wa Wagiriki, nje ya Palestina.

John 7:37

Sasa

Neno "sasa" linatumika hapa kuonyesha mkato ndani ya mstari mkuu wa hadithi.

Siku kubwa

Ni "kubwa" kwa sababu ni ya mwisho, au muhimu zaidi siku ya sikukuu.

Ikiwa yeyote ana kiu

Hii inamaanisha hamu ya mambo ya Mungu, kama vile mwingine anavyoweza kuwa na hamu au "kiu" kwa maji.

Na aje kwangu anywe.

Neno "yeye" maana yake "yeyote." Neno "kunywa" hapa linawakilisha utimilifu wa kiroho katika Kristo.

Maandiko

Hapa "maandiko" linasimama kwa unabii wa Masihi kuhusiana na Kristo. Hii siyo nukuu ya moja kwa moja kutoka fungu lolote maalum la Agano la Kale.

kutiririka ito ya maji ya uzima

Kristo atatoa pumziko la "kiu" ya kiroho kwa watu katika kiwango kikubwa kwamba itatiririkia nje kumsaidia kila aliyepo kama

Maji ya uzima

Hii inamaanisha 1) "maji yatoayo uzima" au "maji yanayowafanya watu kuishi au 2) maji ya asili yatiririkayo kutoka kwenye chemchemi, iliyotofautishwa na maji yatokayo kisimani.

John 7:39

Lakini yeye

"Yeye" inamaanisha Yesu

John 7:40

Nini, Kristo anaweza kutokea Galilaya?

"Kristo hawezi kutoka Galilaya."

Maandiko hayasemi kwamba Kristo atatoka katika ukoo wa Daudi na kutoka Bethlehemu, kijiji alichokuwa Daudi?

"Maandiko yanafundisha kwamba Kristo atatoka katika ukoo wa Daudi na kutoka Bethlehemu, kijiji ambacho Daudi alikuwa."

Maandiko hayajasema?

"Manabii waliandika katika maandiko."

John 7:43

Kukainuka mgawanyiko

Makutano hawakuweza kukubaliana juu ya nani au Yesu alikuwa nani.

Lakini hakuna hata mmoja aliyeinua mkono juu yake

"Lakini hakuna aliyemkamata."

John 7:45

Maafisa

"Walinzi wa Hekalu"

Kwa nini nyinyi hamkumleta?

Hapa "nyinyi" inamaanisha walinzi wa hekalu.

John 7:47

Ndipo Mafarisayo walipowajibu

Hapa "wao" inamaanisha walinzi wa hekalu.

Kupotoshwa

Kudanganywa

Kuna yeyote kati ya watawala aliyemwamini, au yeyote kati ya Mafarisayo?

"Si watawala wala Mafarisayo waliomwamini."

Sheria

Hii ilirejea sheria ya Mafarisayo na si sheria ya Musa.

John 7:50

Sheria yetu humhukumu mtu

Nikodemo alimaanisha kuwa wale wanaoifuata sheria hawamhukumu mtu kabla ya kumhoji.

sheria yetu humhukumu mtu... sivyo?

"Sheria yetu ya Kiyahudi haituruhusu kumhukumu mtu

Na wewe pia unatokea Galilaya?

Inawezekana pia na wewe ni mmoja wa watu wa chini kutoka Galilaya

Hakuna Nabii anayetoka Galilaya

Hii pengine ilirejea katika imani kwamba Masihi hawezi kuzaliwa Galilaya

John 7:53

7:53- 8:11

8:11 Maelezo yaliyotangulia hayana mistari hii.

John 8

Yohana 08 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Watafsiri wanaweza kupenda kuandika alama katika mstari wa 1 ili kuelezea msomaji kwa nini wamechagua kutafsiri au kutotafsiri mistari 8:1-11. Kwa sababu hiki ni kifungu cha utata, ni bora kutokuwa na hitimisho la kitheolojia kutoka kwa kifungu hiki.

Dhana maalum katika sura hii

Mwangaza

Mwangaza ni mfano ya kawaida katika Maandiko yaliyotumiwa kuonyesha haki. Mwangaza pia hutumiwa kuonyesha njia ya haki na kuonyesha maisha ya haki. Giza hutumiwa mara nyingi kama mfano zinazowakilisha dhambi au uovu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#light, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous,

Mimi ndimi

Yohana anatumia maneno haya mara saba katika injili yake. Ni maneno sawa yanayotumiwa na Mungu, alipojidhihirisha pamoja na jina lake Yahweh katika kichaka kilichokuwa kinawaka. Jina "Yahweh" linaweza kutafsiriwa kama "Mimi ndimi."

"Mwanamke aliyekamatwa katika kitendo cha uzinzi"

Ikiwa mwanamke huyo alipatwa katika kitendo cha uzinzi, kulikuwa na mwanamume ambaye pia alikamatwa katika kitendo cha uzinzi. Mwanamume huyo hayuko katika maelezo haya. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#adultery and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Mwana wa Binadamu"

Yesu anajiita mwenyewe kama "Mwana wa Binadamu." Lugha zingine haziwezi kuruhusu mtu kujitaja mwenyewe kama 'mtu wa tatu.'

<< | >>

John 8:1

Watu wote

Watu wengi

Mwanamke aliyekamatwa katika kitendo cha uzinzi

Mwanamke ambaye walimkuta akizini

John 8:4

Sasa katika sheria

"Sasa" ni utangulizi wa kilichotangulia kuwa Yesu na Wayahudi wenye mamlaka walielewa

Watu kama hao

"Watu kama hao" au "watu wafanyao hayo"

Unasemaje kuhusu yeye?

Hii inaweza kutafsiriwa kama amri. "Kwa hiyo tuambie. Tufanyeje kuhusu yeye?"

Kumtega

"Kumtega." Hii inamaanisha kutumia swali la mtego.

Ili kwamba wapate jambo la kumshitaki kwalo

Nini watakachomshitaki nacho inaweza kufanywa wazi. "Ili kwamba wapate kumshitaki kwa kusema jambo baya" au ili kwamba wapate kumshitaki kwa kutoitii sheria ya Musa na sheria ya Warumi.

John 8:7

Wakati walipoendelea

Neno "walipo" linarejea kwa waandishi na Mafarisayo.

Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu

"Kama yeyote kati yenu hana dhambi" au Ikiwa mmoja kati yenu hajatenda dhambi kamwe"

Miongoni mwenu

Yesu alikuwa anaongea na waandishi na Mafarisayo, na pengine makutano ya watu pia.

Mwacheni

Mwacheni mtu huyo

Aliinama chini

Aliinama kufikia chini

John 8:9

Mmoja baada ya mwingine

Mmoja baada ya mwingine

Mwanamke, wako wapi washitaki wako?

Wakati Yesu alipomwita "mwanamke," hakumaanisaha kumdharau au kumfanya ajione mdogo. Ikiwa watu katika makundi yao ya lugha watafikiri kwamba alikuwa akifanya hivyo, hii itafsiriwe bila kutumia neno "mwanamke."

John 8:12

Mimi ni nuru ya ulimwengu

mimi ndiye nitoaye nuru kwa ulimwengu. Maana yake ni kwamba Yesu ameleta ujumbe wa kweli wa Mungu katika ulimwengu uwaokoao wanadamu kutoka giza la dhambi zao.

Ulimwengu

"Watu wa Ulimwengu"

Yeye anifuataye

"Kila mmoja anifuataye." Hii ni njia ya mafumbo isemayo "Kila mmoja atendaye yale ninayofundisha" au " kila mmoja anayenitii."

Uzima

Hii inamaanisha uzima wa kiroho

Unajishuhudia mwenyewe

"Unayasema mambo haya kwa ajili yako mwenyewe."

Ushuhuda wako siyo kweli

"ushuhuda wako siyo kweli" huwezo kuwa shahidi wa kujishuhudia mwenyewe au kile unachokisema juu yako hakiwezi kuwa kweli.

John 8:14

Ingawa najishuhudia mwenyewe

Hata ingawa nasema mambo haya juu yangu binafsi

Mwili

Kanuni za kibinadamu na sheria za watu

Simhukumu yeyote

Maana zuinazowezekana zaweza kuwa 1) Sijamhukumu yeyote bado au 2) Simhukumu yeyote sasa

ikiwa nitahukumu

Ikiwa nitahukumu watu. Maana inawezekana 1) Ninapowahukumu watu ( kwa wakati ujao) au 2) wakati wowote ninapowahukumu watu (sasa) au 3) ikiwa nitahukumu watu.

Hukumu yangu ni kweli

Maana inayowezekana 1) "Hukumu yangu itakuwa sahihi" au 2) Hukumu yangu ni sahihi

Siko peke yangu, lakini niko pamoja na Baba aliyenituma

Yesu, Mwana wa Mungu, anayo mamlaka kwa sababu ya uhusianomwake maalumu na Baba yake, aliyemtuma. Neno "Baba" na "Mwana" linaonyesha uhusiano wa watu wa Mungu kati yao.

Siko peke yangu

Siko peke yangu katika hukumu. "Siko peke yangu jinsi ninavyohukumu" au "sihukumu peke yangu."

Niko pamoja na Baba

"Baba pia anahukumu pamoja na mimi" au "Baba anahukumu kama nihukumuvyo mimi."

Baba

Hiki ni cheo maalumu kwa Mungu

Baba aliyenituma

Neno "aliyenituma" inazungumza jambo zaidi kuhusu Baba. "Baba, yeye pekee aliyenituma."

John 8:17

Ndiyo, na katika sheria yenu

Neno "Ndiyo" inaonyesha kwamba Yesu anaongeza kile alichosema kabla.

Imeandikwa

Musa aliandika

Ushuhuda wa watu wawilini kweli

"Ikiwa watu wawili watasema jambo lile lile, ndipo watu watakapojua ni kweli"

John 8:19

Hamnijui mimi wala Baba yangu, kama mngelinijua mimi, mngelimjua na Baba yangu vile vile."

Yesu anaonyesha kwamba kumjua yeye ni kumjua Baba pia. Wote Baba na Mwana ni Mungu mmoja, kwa hiyo kumjua mmoja ni kuwajua wote.

Baba yangu

Hiki nicheo muhimu kwa Mungu.

John 8:21

Kufa katika dhambi zenu

"Kufa wakati ukiwa mwenye dhambi." au "utakufa wakati ukiendelea kutenda dhambi." Hapa neno "Kufa" linaelezea kifo cha kiroho.

Hauwezi kuja

"Hauna uwezo wa kuja"

Je atajiua mwenyewe, yeye aliyesema

Hii yaweza kutafsiriwa kama maswali mawili yaliyotenganishwa. Atajiua mwenyewe? Hivyo ndiyo sababu anasema"

John 8:23

isipokuwa uamini kwamba MIMI NDIYE, utakufa

Ikiwa hautaamini

kwamba MIMI NDIYE

Kwamba mimi ni Mungu

John 8:25

Walisema

Neno hili linamaanisha viongozi wa Kiyahudi

Baba

Baba yake

John 8:28

Utakapoinuliwa juu

Utakapoinuliwa. Hili halijatokea bado.

Mwana wa Mtu.... Baba

Hivi ni vyeo muhimu vinavyoelezea uhusiano wa Yesu na Mungu.

MIMI NDIYE...BABA alinifundisha

kama Mungu Mwana, anavyomjua Mungu Baba tofauti na mwingine yeyote, na divyo ilivyo wakati wote

Kama Baba alivyonifundisha

katika njia ile ile kwamba Baba alinifundisha

Yeye aliyenituma

Neno linamaanisa Baba

Kama Yesu alivyosema

wakati Yesu alipokuwa akisema

John 8:31

baki katika neno langu

Tii kile nilichosema

kweli itakuweka huru

Ikiwa mtautii ukweli, Mungu atawaweka huru"

John 8:34

Amini, amini

Tafsiri hii kama ilivyofanyika Yoh. 1:49

Ni mtumwa wa dhambi

"Ni kama mtumwa wa dhambi." Hii inamaanisha kwamba dhambi ni kama bwana wa mwenye dhambi.

Katika nyumba

Nyumbani mwa

Ikiwa Mwana atawaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli

Kulingana na tamaduni zao, mwana mkubwa anaweza kumweka huru mtumwa katika nyumba yake.

Mwana

Hiki ni cheo muhimu kwa Yesu, Mwana wa Mungu.

John 8:37

Neno langu

Mafundisho yangu

John 8:39

Baba

Mababa

Ibrahimu hakufanya hili

Ibrahimu kamwe hakujaribu kumwua yeyote aliyemwambia ukweli kutoka kwa Mungu

Hatukuzaliwa katika dhambi ya zinaa

Wote tulizaliwa kutoka ndoa sahihi

John 8:42

Pendo

Huu ni aina ya upendo unaotoka kwa Mungu na unaelekea katika mema ya wengine, hata kama haufaidiki chochote.

Kwa nini hamyaelewi maneno yangu?

Yesu anatumia swali hili hasa hasa kuwakemea viongozi wa Kiyahudi kwa kutomsikiliza yeye.

John 8:45

Nani kati yenu ananishuhudia kuwa ni mwenye dhambi?

Hakuna yeyote kati yenu anayeweza kunishuhudia kuwa mimi nina dhambi." Yesu aliuliza swali hili kuweka mkazo kuwa yeye hana dhambi.

Kwa nini haniamini

Hamna sababu ya kushindwa kuniamini" Yesu alitumia swali hili kuwakemea viongozi wa Kiyahudi kwa kutoamini kwao.

John 8:48

Wayahudi

Neno Wayahudi linatumika kuwakilisha viongozi wa Kiyahudi.

John 8:50

Kuyashika maneno yangu

Tii kile ninachosema

Kifo

Hii inamaanisha kifo cha kiroho

John 8:52

Baba

Mababa

John 8:54

Ni Baba yangu anayenitukuza

Hakuna mwanadamu amjuaye Mungu Baba kama Mungu Mwana, Yesu Mwana wa Mungu. Mungu Baba humtukuza Mwana kwa sababu wote Baba na Mwana ni Mungu wa milele.

Baba

Hiki ni cheo muhimu kwa Mungu

John 8:57

Haujafikisha bado umri wa miaka hamsini, na umeshamuona Ibrahimu?

Miaka yako ya umri ni chini ya hamsini. Usingelikuwa umemuona Ibrahimu."

Amini, amini

Tafsiri hii kama ulivyofanya katika Yoh. 1:49

John 9

Yohana 09 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

"Ni nani aliyetenda dhambi?"

Katika Israeli ya kale, mara nyingi waliamini kwamba mtoto alizaliwa na ulemavu kwa sababu ya dhambi ya mmoja wa wazazi wake. Hii haikuwa mafundisho ya sheria ya Musa. Katika mjadala huu, Mafarisayo walikuwa wenye dhambi kwa sababu waliona uwezo wa Yesu na hawakumuabudu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lawofmoses).

Mimi mdimi

Yohana anatumia maneno haya mara saba katika injili yake. Ni maneno sawa yanayotumiwa na Mungu, alipojidhihirisha pamoja na jina lake Yahweh katika kichaka kilichokuwa kinawaka. Jina "Yahweh" linaweza kutafsiriwa kama "Mimi ndimi."

Mwangaza

Mwangaza ni mfano wa kawaida katika Maandiko yaliyotumiwa kuonyesha haki. Mwangaza pia hutumiwa kuonyesha njia ya haki na kuonyesha maisha ya haki. Giza hutumiwa mara nyingi kama mfano unaonyesha dhambi au uovu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#light, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#darkness, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#unrighteous)

"Yeye haishiki Sabato"

Mafarisayo walimwona Yesu akifanya matope kuwa "kazi" na kukiuka sheria kuhusu Sabato. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sabbath)

Mifano muhimu ya usemi katika sura hii

Kuona

Katika sura hii kumeandikwa habari ya mtu aliyezaliwa kipofu. Yesu pia anatumia habari hizi kama mfano. Katika Yohana 9:39-40, Mafarisayo wanaitwa vipofu kwa sababu hawawezi kuona ukweli ulio mbele yao. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Mwana wa Binadamu"

Yesu anajiita mwenyewe kama "Mwana wa Binadamu." Lugha zingine haziwezi kuruhusu mtu kujitaja mwenyewe kama 'mtu wa tatu.' (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sonofman)

<< | >>

John 9:1

Yesu alipopita karibu

hapa inamaanisha Yesu na wanafunzi wake

John 9:3

Sisi

Neno sisi linawahusisha wote Yesu na wanafunzi wake aliokuwa akiongea nao.

Mchana...Usiku

Yesu analinganisha wakati watu wanaweza kufanya kazi wakait wa mchana, wakati ambao kwa kawaida watu hutenda kazi, na wakati wa usiku watu hawawezi kufanya kazi ya Mungu.

Nuru ya Ulimwengu

Yule ambaye aonyeshaye kile kilicho cha kweli kama vile nuru ionyeshacho kilicho halisi.

John 9:6

alifanya udongo kwa kutumia mate

Yesu alitumia vidole kuchanganya udongo na mate.

aliosha

aliosha macho yake kwenye kisima

John 9:8

Huyu siye mtu....mwombaji?

Huyu mtu ni yule ... omba, siyo yeye? au "Huyu ni mtu... omba. Ndiyo ni yeye.

John 9:10

alipakwa... macho

Angalia jinsi ulivyotafsiriwa Yoh. 09:06

John 9:13

siku ya Sabato

Siku ya mapumziko kwa Wayahudi

John 9:16

Hawezi kutunza sabato

Hii inamaanisha kuwa hakutii sheria kuhusu Sabato.

Ishara

Miujiza pia yaweza kuitwa ishara kwa sababu imetumika kama viashirio au ushahidi kwamba Mungu ana uwezo wote aliye na mamlaka kamili juu ya ulimwengu.

John 9:19

Waliwauliza wazazi

hapa inamaanisha viongozi wa Wayahudi

yeye ni mtu mzima

yeye ni mwanaume au yeye si mtoto tena

John 9:22

Hofu

Hii inamaanisha hisia zisizokuwa mzuri anazokuwa nazo mtu kama kuna utisho au madhara kwake au kwa wengine

John 9:24

Walimwita mtu

Hapa, "Walimwita" walimaanisha Wayahudi.

Mtu huyu

Hili linarejea kwa Yesu

Mtu yule

Hili linarejea kwa mtu aliyekuwa kipofu

Awe ni mwenye dhambi, mimi sijui

Sijui kama ni mwenye dhambi au la

John 9:26

Sentensi unganishi:

Wayahudi wanaendelea kuongea na mtu aliyekuwa kipofu

Kwa nini mnataka kusikia tena?

Kauli hii ipo katika mfumo wa swali kuelezea kushangazwa kwa yule mtu aliyeponywa awaelezee tena kuhusu kilichotokea.

John 9:30

Hawasikilizi wenye dhambi...humsikiliza

"Hajibu maombi ya mwenye dhambi...Mungu hujibu maombi yake."

John 9:32

Haijasikiwa kamwe kwamba mtu amefungua macho ya mtu aliyezaliwa kipofu

"Hakuna aliewahi kusikia mtu amefumbua macho"

Ikia mtu huyu hakutoka kwa Mungu, asingefanya chochote

"Ikiwa mtu huyu hakutoka kwa Mungu, asingefanya chochote, lakini ameniponya, kwa hiyo yamkini ametoka kwa Mungu."

ulizaliwa katika dhambi, na wewe sasa unataka kutufundisha sisi?

"Ulizaliwa kamili katika dhambi. Hauna sifa za kutufundisha.

John 9:35

Kuamini

Hii in maana ya kumwamini Yesu, kuamini kwamba, ni Mwana wa Mungu, kumtumaini yeye kama Mwokozi, na kuishi katika njia iletayo heshima kwake.

John 9:39

Ili kwamba wale wasioweza kuona wapate kuona na kwamba wale wanaoona wawe vipofu.

Ili kwamba wale wasioona kwa macho yao wapate kumtambua Mungu na ili kwamba wale ambao wanaona kwa macho yao wasimtambue Mungu.

John 10

Yohana 10 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Kondoo

Kondoo ni taswira ya kawaida inayotumiwa kutaja watu. Katika kifungu hiki, inahusu hasa watu wanaoamini Yesu na kumfuata. Mafarisayo pia wanalinganishwa na mbwa mwitu wanaoiba na kuharibu kondoo.

Kufuru

Ikiwa mtu hujiita Mungu, basi inachukuliwa kuwa ni kufuru. Katika sheria ya Musa, adhabu ya kufuru ilikuwa kupigwa mawe hadi kufa. Hawakuamini Yesu, kwa hiyo wakachukua mawe ili wamwue. Yesu hakuwa na hatia ya kufuru kwa sababu yeye ni Mungu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#blasphemy and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lawofmoses)

Mifano muhimu ya usemi katika sura hii

Zizi la kondoo

Mfano uliotumiwa hapa ni kuhusu mahali ambapo kondoo huchungwa. Kungekuwa na mlango au lango ambalo mchungaji angekuwa ameingia ndani ya zizi la kondoo. Kondoo mara moja humtambua. lakini, wizi angeingia ndani ya zizi la kondoo kwa njia nyingine ambayo hawezi kukamatwa. Kondoo watakimbia kutoka mwizi kwa sababu hawakumtambua. Yesu anatumia hii kama mfano wa huduma yake. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

"Ninatoa maisha yangu ili niipate tena"

Ingawa maneno haya hakuwekwa tofauti na mengine, lakini hakika ni unabii uhusu kifo cha Yesu. Inasisitiza kwamba kwa hiari alikufa kwa ajili ya dhambi za mwanadamu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#prophet and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

<< | >>

John 10:1

Amini, amini

Itafsiriwe kama ilivyofanyika katika Yoh. 1:49

zizi la kondoo

Hili ni eneo lenye uzio sehemu ambayo mchungaji huwatunza kondoo wake.

Mwizi na mnyang'anyi

Hili ni tumizi la maneno mawili yanayofanana ili kuongeza mkazo

John 10:3

mlinzi wa geti

huyu ni mtu aliyeajiriwa kulinda getini wakati wa usiku

kondoo husikia sauti yake

kondoo husikia na kuelewa sauti yake

John 10:5

Hawakuelewa

Maana inayowezekana: 1) "Wanafunzi hawakuelewa" au 2) Makutano hawakuelewa." Unaweza pia kuiacha kama "hawakuelewa>"

John 10:7

Amini, amini

Tafsiri kama ulivyofanya katika Yoh. 1:49

Mimi ni mlango wa kondoo

"Mimi ni njia wanayoipitia kondoo kwenda zizini." Yesu anasema yeye ndiye anayeruhusu kuingia. Neno "kondoo" limetumika kumaanisha watu wa Mungu.

Wote waliokuja kabla yangu

Hili linarejea kwa walimu wengine waliofundisha kabla ya Yesu.

wezi na wanyang'anyi

Yesu anawaita "wezi na wanyang'anyi" kwa sababu mafiundisho yao yalikuwa ya uongo, na walikuwa wakkijaribu kuwaongoza watu wa Mungu wakati hawaujui ukweli.

John 10:9

Mimi ni mlango

Alimaanisha yeye mwenyewe kama "mlango," Yesu anaonyesha kwamba anatoa njia ya kweli kupata kile zizi la kondoo linawakilisha.

Malisho

Neno "malisho" linamaanisha eneo lenye nyasi mahali kondoo huenda kula.

Hawezi kuja isipokuwa

Hiki ni kinyume mara mbili. Katika lugha zingine ina uasilia zaidi kwa kutumia sentensi chanya.

Ili kwamba wawe na uzima

Neno "wawe" linamaanisha kondoo. "uzima" linamaanisha uzima wa milele.

John 10:11

Mimi ni mchungaji mwema

Mimi nafanana na mchungaji mwema

Huyatoa maisha yake

Kuweka kitu chini maana yake kuondoa uwezo wake. Ni lugha laini yenye kumaanisha kufa.

John 10:14

Mimi ni mchungaji mwema

Mini nafanana na mchungaji mwema

Baba ananijua mimi, nami namjua Baba

Mungu Mwana na Mungu Baba (na Mungu Roho Mtakatifu) wanafahamiana na wote ni nafsi ya Mungu.

Baba

Hiki ni cheo maalumu cha Mungu

Zizi

Kundi la kondoo linalomilikiwa na mchungaji. Neno hili linatokana na neno "Zizi" mahali ambapo kondoo hukaa.

Nautoa uhai wangu kwa ajili ya kondoo

Hii ni njia ya upole ya Yesu kusema kwamba atakufa ilikuwalinda kondoo. "Ninakufa kwa ajili ya kondoo."

John 10:17

Anapenda

Aina hii ya upendo hutoka kwa Mungu, na unaelekezwa kwa ajiliya mema ya wengine, hata kama haimfaidii mtu binafsi. Aina hii ya upendo huwajali wengine, haijalishi wamefanya nini.

Hii ndiyo sababu Baba ananipenda: Nami nautoa uhai wangu

Mpango wa Mungu wa milele ulikuwa kwa Mungu Mwanakuutoa uhai wake ili kulipa kwa ajili ya dhambi za wanadamu. Kifo cha Yesu Msalabani unafunua wenye nguvu wa Mwana kwa Baba na wa Baba kwa Mwana.

Baba

Hiki ni cheo maalumu cha Mungu.

Ninayatoa maisha yangu ili kwamba nipate kuyatwaa tena

Hii ni njia ya upole ya Yesu kusema atakufa na baadaye kuwa mzima tena. "Najiruhusu mwenyewe kufa ili kwamba ninaweza kujirudisha kuwa mzima tena.

John 10:19

Kwa nini mnamsikiliza?

"Msimsikilize"

Je pepo laweza kufumbua macho ya aliyekuwa kipofu?

"Pepo hawezi kumfanya kipofu apate kuona."

John 10:22

Sikukuu ya kuwekwa wakfu

Hii ni siku ya nane, mapumziko ya wakati wa baridi Wayahudi huitumia kukumbuka muujiza wa Mungu alipofanya mafuta kidogo kubaki katika taa mpaka walipopata mafuta mengine baada ya siku nane baadaye. Taa ilitumika kuweka wakfu hekalu la Kiyahudi kwa Mungu. kuweka wakfu kitu ni ahadi ya kukitumia tu kwa kusudi maalumu.

kibaraza

Huu ni muundo uliounganishwa na jengo, ina paa na inaweza kuwa na ukuta ama isiwe nao.

John 10:25

Katika jina la Baba yangu

Hii inamaanisha kuwa Yesu alifanya mambo haya kwa uwezo na mamlaka ya Baba yake. Yesu ni mkamilifu , mtakatifu Mwana w Mungumwenye uwezo wa milele kutoka kwa Baba ili kulipa kwa ajili ya dhambi zote milele na kuokoa na kuwasamehe wote waliomwamini.

Haya yanashuhudia kuhusu mimi

Miujiza yake ilithibitisha kuhusu yeye kama vile shahidi anavyoshuhudia mahakamani.

Siyo kondoo wangu

"Siyo wafuasi wangu" au "siyo wanafunzi wangu" au "siyo watu wangu"

John 10:29

Baba yangu...amewatoa kwangu...hakuna aliye na uwezo wa kuwanyakua kutoka mkononi mwa Baba.

Mungu Baba na Mungu Mwana kwa uwezo wao huwalinda waliookoka.

Baba yangu

Hiki ni cheo uhimu kwa Mungu

Mkono wa Baba

Neno "mkono" linatumika kumaanisha umiliki wa Mungu au madaraka na ulinzi wake.

Mimi na Baba yangu tu umoja

Yesu, Mungu Mwana,na Mungu Baba ni umoja. Wao ni nafsi za Mungu mmoja na wa kweli (pamoja na Roho). Wana umoja katika makusudi, uwezo, mamlaka, huruma na utakatifu. Wao ni Mungu.

John 10:32

Yesu aliwajibu, "Nimeshawaonyesha kazi nyingi nzuri kutoka kwa Baba

Kazi za Yesu zilifanyika katika uwezo wake kama Mwana wa Mungu, katika umoja na Mungu Baba. Kazi za Yesu ni kazi za Baba vile vile (na Roho Mtakatifu).

Baba

Hiki ni cheo muhimu kwa Mungu

Unajifanya kuwa Mungu

"Alidai kuwa yeye ni Mungu"

Tuna...kuponda mawe kwa...kukufuru, kwa sababu wewe, uliye mtu, unajifanya kuwa Mungu

Yesu alidai kuwa yeye ni Mwana wa Mungu ilikuwa ni kufuru kwa Wayahudi kwa sababu walidhani kuwa Yesu alikuwa akidai kuwa yeye ni Mungu - na ndivyo alivyokuwa.

John 10:34

Ninyi ni miungu

Kwa kawaida neno "mungu" huonyesha "mungu wa uongo" vinginevyo iwe imeandikwa kwa herufi kubwa "M," imaanishayo kwa mmoja Mungu wa kweli. Lakini hapa, Yesu ananukuu maandiko mahali Mungu anawaita wafuasi wake "miungu" kwa sababu amewachagua kumwakilisha duniani.

Je haikuandikwa...miungu?

"Mnapaswa kujua tayari kuwa imeandikwa...miungu"

Maandiko hayawezi kuvunjwa

Maana inayowezekana ni 1) "hakuna atakayebadilisha maandiko." 2) "Maandiko yataendelea kuwa kweli."

'Unakufuru; kwa sababu nilisema, mimi ni Mwana wa Mungu

Wapinzani wa Yesu waliamini kuwa Yesu alikuwa anakufuru alipojiita "Mwana wa Mungu" kwa sababu kusema hivyo ilikuwa ni kudai kuwa sawa na Mungu.

Baba... Mwana wa Mungu

Hivi ni vyeo muhimu vinavyoelezea uhusiano kati ya Mungu na Yesu

John 10:37

Baba

Hiki ni cheo muhimu kwa Mungu

Niaminini

Hapa neno "amini" maana yake ni kukubali au kutumaini kile ambacho mtu huyo amesema ni cha kweli.

Ziaminini kazi

Hapa "Zizminini" maana yake kutumaini kuwa kitu ni cha kweli na kutenda kwa njia hiyo inayoonyesha imani hiyo.

Baba yu ndani yangu na kwamba mimi ni ndani ya Baba

Mungu Baba yuko ndani ya Yesu, Mwana wa Mungu, kwa sababu Mungu Mwana yu ndani ya Baba. Kama nafsi za Mungu, Baba na Mwana wote ni Mungu mmoja wa milele, pamoja na Mungu Roho.

mkono wao

"ufahamu wao." Hii maana ya ke ni kuwa katika nafasi isiyo salama anapoweza kukamatwa.

John 10:40

Yohana kweli hakufanya ishara, lakini mambo yote ambayo Yohana alisema juu ya mtu huyu ni ya kweli.

Ni kweli kwamba Yohana hakufanya ishara, lakini aliongea ukweli juu ya huyu mtu, anayefanya ishara.

Ishara

Miujiza inayothibitisha kwamba kitu fulani ni cha kweli au kinachompa mwingine kuwa na kibali

John 11

Yohana 11 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Mwangaza

Mwangaza ni mfano ya kawaida katika Maandiko yaliyotumiwa kuonyesha haki. Mwangaza pia hutumiwa kuonyesha njia ya haki na kuonyesha maisha ya haki. Giza hutumiwa mara nyingi kama mfano wa kuonyesha dhambi au uovu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#light, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#darkness, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#unrighteous)

Mimi ndimi

Yohana anatumia maneno haya mara saba katika injili yake. Ni maneno sawa yanayotumiwa na Mungu, alipojidhihirisha pamoja na jina lake Yahweh katika kichaka kilichokuwa kinawaka. Jina "Yahweh" linaweza kutafsiriwa kama "Mimi ndimi."

Pasaka

Sura hii inaeleza kuwa Yesu hakutembea tena waziwazi kati ya Wayahudi. Kwa hiyo, Mafarisayo walisubiri kumtafuta wakati wa Pasaka. Ilikuwa ni wajibu wa Wayahudi, waliokuwa na uwezo, kwenda Yerusalemu wakati wa sherehe ya Pasaka. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#passover)

Mifano muhimu ya usemi katika sura hii

"Mtu mmoja anapaswa kufa kwa ajili ya watu"

Kayafa akasema, "Ni vyema kwenu kwamba mtu mmoja afe kwa ajili ya watu badala ya kuwa taifa lote lipotee." Ni ajabu kwamba Yesu angekuja kufa kwa ajili ya dhambi za taifa na ulimwengu wote. Maneno haya ni kama unabii kuhusu kifo cha Yesu kwa ajili ya dhambi. Hiki ni kitu ambacho kuhani mkuu pia anatabiri kuhusu baadaye katika sura hii. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-irony and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#prophet)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Kama ungalikuwa hapa"

Maria na Martha walimwamini Yesu lakini hawakuelewa kikamilifu yeye ni nani. Katika kifungu hiki, hawakutambua kwamba alikuwa na nguvu juu ya kifo yenyewe na angeweza kumfufua Lazaro kutoka kwa wafu ikiwa angependa. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

<< | >>

John 11:1

Maelezo ya jumla:

Hii ni habari inayomhusu Lazaro. Mistari hii inamtambulisha yeye na kutoa historia fupi juu yake na dada yake Mariamu.

Ni Mariamu ndiye aliyempaka Bwana mafuta...nywele zake

Yohana pia anamtambulisha Mariamu, dada yake na Matha.

John 11:3

aliomba Yesu aje

"alitaka Yesu aje kwake"

upendo

Hapa "upendo" inamaanisha upendo wa ndugu, wa asili, upendo wa kibinadamu kati ya marafiki na ndugu.

Kifo

Hii inamaanisa kifo cha kimwili

badala yake kwa utukufu wa Mungu ili kwamba Mwana wa Mungu apate kutukuzwa katika hilo

Yesu kama Mwana wa Mungu, amepokea utukufu ule ule kama wa Mungu

Mwana wa Mungu

Hili ni jina muhimu kwa Yesu

John 11:5

Sasa Yesu alimpenda Martha na dada yake pamoja na Lazaro

Haya ni maneno ya utangulizi

John 11:8

Rabi, Wayahudi walikuwa sasa wanatafuta kukuponda mawe, na unarudi tena huko?

"Mwalimu, kwa hakika huhitaji kurudi huko! Wayahudi wanajaribu kukuponda mawe.!"

Je hakuna masaa kumi na mbili ya mchana?

"Unajua kwamba siku ina masaa kumi na mbili za mchana

John 11:10

Nuru haimo ndani yake

Maana halisi 1) "hawezi kuona" au 2) hawezi kuona"

Rafiki yetu Lazaro amelala

Lazaro amekufa lakini kwa ajili ya muda mfupi tu.

Lakini ninaenda ili kwamba nipate kumwamsha kutoka usingizini

Yesu anaufunua mpango wake wa kumfufua Lazaro.

John 11:12

Maelezo ya jumla

Katika mustari wa 13 kuna kituo katika mtiririko wa habari kama ambavyo Yohana unaongelea kuhusu wanafunzi wa Yesu kutokuelewa kile ambacho Yesu alimaanisha aliposema kuwa Lazaro amelala.

kama amelala

Wanafunzi walidhani kuwa Lazaro amepumzika tu na baadaye ataamka.

John 11:15

Sentensi unganishi:

Yesu anaendelea kuongea na wanafunzi wake

kwa ajili yenu

kwa faida yenu

John 11:17

Maelezo ya jumla:

Kwa sasa Yesu yupo Bethania.

alimkuta Lazaro tayari alikuwa kaburini kwa muda wa siku nne

Unaweza kutafasiri hivi pia, "alijua kwamba watu walikuwa wamekwisha kumweka Lazaro kaburini kwa muda wa siku nne kabla ya yeye kufika"

kuhusiana na kaka yao

Lazaro alikuwa kaka yao mdogo

John 11:21

Kaka yangu asingalikufa

"Kaka yangu angeendelea kuwa mzima"

Fufuka tena

Maana yake kumfanya mtu aliyekufa kuishi tena

John 11:24

Ajapokufa

Hapa "kufa" inamaanisha kifo cha kimwili

Bado ataishi

Hapa "Ishi" linamaanisha uzima wa kiroho

Naye aishiye na kuniamini hatakufa kamwe

Na wote waniaminio mimi hawatatengwa kamwe milele kutoka kwa Mungu.

Hatakufa kamwe

Hapa "kufa" inamaanisha kifo cha kiroho

John 11:27

Ndiyo, Bwana, ninaamini kwamba wewe ni Kristo, Mwana wa Mungu, yeye... ajaye katika ulimwengu.

Martha aliamini kwamba Yesu ni Bwana, Kristo (Masihi), Mwana wa Mungu.

Mwana wa Mungu

Hiki ni cheo maalumu cha Yesu.

Mwalimu

Cheo hiki kinamhusu Yesu

John 11:30

Anguka chini ya miguu yake

Mariamu alilala chini au alipiga magoti katika miguu ya Yesu kuonyesha heshima

Kama ungelikuwa hapa, kaka yangu asingelikufa

Angalia hili ulivyotafsiri katika Yoh. 11:21

John 11:33

alisikitika sana moyoni mwake na roho yake iliumia

Yohana anatumia sentensi hizi mbili kuelezea uzito wa maumivu ya moyo ambayo Yesu aliyapata.

Mme mweka wapi

Hii ni njia nyingine ya kuuliza, "mmemzika wapi?"

Yesu akalia

Yesu alianza kulia

John 11:36

Mpendwa

Hili linamaanisha juu ya upendo wa ndugu au upendo wa kibinadamu kwa rafiki au mtu wa familia.

isingefaa huyu mtu, aliyefungua macho ya yule aliyekuwa kipofu, hakuweza kumfanya mtu huyu asife?

Aliweza kumponya mtu aliyekuwa kipofu, kwa hiyo angeweza pia kumponya mtu huyu ili kwamba asife." au "Hakuweza kumfanya mtu huyu asife, kwa hiyo tunajua kuwa hakumponya kweli mtu aliyezaliwa kipofu kama wanavyosema alifanya."

Kufungua macho

Kuponya macho

John 11:38

Je sikusema kwamba, ikiwa utaamini, utauona utukufu wa Mungu?

"Kumbuka kwamba nilikuambia, ikiwa utaniamini, utaona ni kwa jinsi gani Mungu ni Mkuu

mpaka muda huu mwili wake utakuwa umeoza

mpaka muda huu kutakuwa na harufu mbaya

John 11:41

Baba, ninakushukuru kwamba umenisikiliza

Yesu alikuwa akiomba moja kwa moja kwa Baba kama ushuhuda kwa waliokuwa pamoja naye

Baba

Hiki ni cheo maalumu kwa Mungu

John 11:43

Amefungwa mikono na miguu kwa nguo za kuzikia, na uso wake ulikuwa umefungwa kwa nguo.

Utamaduni wa kuzika kwa wakati huu ulikuwa wa kuufunga mwili wa marehemu kwa nguo ndefu za kitani

Yesu aliwaambia

Neno "wao" linamaanisha juu ya watu waliokuwa pale na kuona muujiza.

John 11:45

Maelezo ya jumla

Mistari hii inatuambia mambo yaliyotokea baada ya Lazaro kufufuliwa kutoka wafu.

John 11:47

Maelezo ya jumla

Hii ni sehemu ya pili ya simulizi. Kuhani mkuu pamoja na Mafarisayo wanakutana kwa ajili ya kikao cha baraza la Kiyahudi

Kisha makuhani wakuu

kisha viongozi kati ya makuhani

wote wataishi ndani yake

Viongozi wa Kiyahudi waliogopa kwamba watu wangemfanya Yesu kuwa mfalme wao.

John 11:49

Haujui chochote kabisa

"Hauelewi ni itu gani kinatendeka" au Haujui nini cha kufanya lakini mimi najua."

mtu mmoja kati yao

Hii ni njia ya kumtambulisha mhusika mpya katika simulizi.

John 11:51

kufa kwa ajili ya taifa

Neno "taifa" linatumika kuonyesha watu wa taifa la Israel.

Watoto wa Mungu

Hili linamaanisha watu wa Mungu kwa njia ya imani katika Yesu na ni watoto wake wa kiroho.

John 11:54

Maelezo ya jumla:

Yesu anaondoka Bethania na kwenda Efraimu.

tembea kwa uhuru mbele ya Wayahudi

Hapa anaongelea viongozi wa Kiyahudi.

nchi

hili ni eneo nje ya mji ambapo watu wachache wanaishi.

John 11:56

Walikuwa wakimtafuta Yesu

Neno "Walikuwa" linawazungumza Wayahudi waliosafiri kuja Yerusalemu.

Unafikiri nini? Kwamba hawezi kuja katika sikukuu?

Mzungumzaji hapa alikuwa akishangaa ikiwa Yesu atakuja katika sikukuu ingawa kulikuwa na hatari ya kukamatwa. Aliwauliza wengine waliomzunguka kuhusiana na mawazo yao. "Mnafikiri Yesu anaweza kuwa woga sana kuja katika sikukuu?"

Sasa wakuu wa makauhani

Haya ni maelezo ya nyuma ambayo yanaelezea kwa nini waabudu wa Kiyahudi walikuwa wakishangaa ikiwa Yesu atakuja katika sikukuu au la. Ikiwa lugha yako inayo njia ya kuweka alama ya maelekezo ya nyuma fanya hivyo.

John 12

Yohana 12 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri hupendelea kuweka nukuu za Agano la Kale. Tafsiri ya ULB na nyingine nyingi za Kiingereza huingiza mistari ya 12:38 na 40, ambayo ni nukuu kutoka Agano la Kale.

Mstari wa 16 ni ufafanuzi juu ya matukio haya. Inawezekana kuweka mstari huu mzima kwa mabano ili kuonyesha tofauti na maelezo ya habari.

Dhana maalum katika sura hii

Upako

Ilikuwa ni desturi kupaka mafuta mwili katika maandalizi ya kuizika. Hii kwa kawaida haingefanyika mpaka baada ya kifo cha mtu. Hii haikuwa nia ya Maria. Yesu anatumia matendo ya Maria kutabiri kuhusu kifo chake kilichokuwa kinakaribia. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#anoint, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#prophet and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

Punda

Jinsi ambavyo Yesu aliingia Yerusalemu, akiwa amepanda mnyama, ilikuwa sawa na vile ambavyo mfalme angeingia katika mji baada ya ushindi mkubwa. Na kwa wafalme wa Israeli, ilikuwa desturi kupanda punda badala ya farasi. Mathayo, Marko, Luka, na Yohana wote waliandika juu ya tukio hili, lakini hawakupa maelezo sawa. Mathayo aliandika kuhusu kuwepo kwa punda na mwana-punda, lakini haijulikani ni yupi ambaye Yesu alipanda. Ni bora kutafsiri kila moja ya vifungu hivi kama inavyoonekana katika ULB bila kujaribu kuwafanya wote kusema jambo sawa. (Angalia: Mathayo 21: 1-7 na Marko 11: 1-7)

Mwangaza

Mwangaza ni mfano ya kawaida katika Maandiko yaliyotumiwa kuonyesha haki. Mwangaza pia hutumiwa kuonyesha njia ya haki na kuonyesha maisha ya haki. Giza hutumiwa mara nyingi kama mfano ya kuonyesha dhambi au uovu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#light, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#darkness, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#unrighteous)

Mifano muhimu ya usemi katika sura hii

"Ili atukuzwe"

Unabii wa Yesu kuhusu kutukuzwa kwake ni maelezo juu ya kifo chake. Wanafunzi hawakuelewa kwamba kifo chake kingemtukuza, lakini kilifanyika vivyo hivyo. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#glory and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-irony)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Kitendawili

Kitendawili ni taarifa inayoonekana kuwa ya ajabu, ambayo ni kana kwamba inajikana yenyewe, lakini kwa hakika sio ya ajabu. Kitendawili kinatokea katika 12:25: "Yeye anayependa maisha yake ataipoteza, lakini anayechukia maisha yake katika ulimwengu huu ataichunga kwa uzima wa milele." Lakini katika 12:26 Yesu anaelezea maana ya kuchunga maisha ya mtu kwa ajili ya uzima wa milele. (Yohana 12: 25-26).

<< | >>

John 12:1

Litra

Litra ni kipimo cha uzito - paundi ya Kirumi ni sawa na gramu 327.5

Manukato

Hiki ni kimiminika chenye harufu nzuri kilichotengezwa kwa mafuta ya miti na maua yanayonukia vizuri.

nardo

Haya ni manukato yaliyotengenezwa kutokana na maua yanayopatikana katika milima ya Nepali, China, na India.

nyumba yote ilijaa harufu ya manukato

"harufu nzuri ya manukato yake iliijaza nyumba"

John 12:4

yeye ambaye angemsaliti Yesu

"Yeye ambaye baadaye aliwasaidia maadui wa Yesu kumkamata"

Basi alisema hivi...chukua baadhi ya vilivyomo ndani kwa ajili yako

Yohana anaeleza kwanini Yuda aliuliza swali kuhusu maskini.

aliyasema haya, sio kwasababu aliwahurumia maskini, bali kwasababu alikuwa mwizi

"alisema hivi kwasababu alikuwa mwizi. Hakuwajali maskini"

John 12:7

mwache atunze alicho nacho kwa ajili ya siku ya maziko yangu

Yesu anaeleza kuwa matendo ya yule mwanamke yanaweza kueleweka kama tazamio la kifo na maziko yake

maskini mtakuwa nao siku zote

Yesu anamaanisha kuwa mtakuwa na nafasi ya kuwasaidia maskini siku zote

lakini hamtakuwa na mimi siku zote

Kwa njia hii Yesu anasema kwamba atakufa

John 12:9

Basi

Neno hili limetumika hapa kuonesha kituo katika simulizi. Hapa Yohana anaelezea kundi jipya la watu katika simulizi.

kwasababu yake

Ukweli kwamba Lazaro alikuwa hai kulisababisha Wayahudi wengi wamwamini Yesu.

Walimwamini Yesu

Hii inamaanisha "walimwamini Yesu"; hivi, waliamini kuwa yeye ni Mwana wa Mungu, kumwamini yeye kama Mwokozi, na kuishi kwa kumheshimu yeye.

John 12:12

Hosana

Hii inamaanisha "Mungu aokoe."

Mbarikiwa

Hii huelezea hamu ya kutaka Mungu afanye mambo mazuri kwa mtu huyo.

ajae kwa jina la Bwana

Kuja kwa jina la mtu fulani humaanisha kutumwa kwa mamlaka na nguvu zake, au kuja kama mwakilishi wake.

John 12:14

binti Sayuni

"Binti Sayuni" ni neno linalomaanisha Israeli, kama vile "wana wa Israeli" au "watu kutoka Yerusalemu."

kama ilivyoandikwa

Unaweza kutafasiri hivi, "kama ambavyo manabii waliandika katika maandiko."

John 12:16

wakati Yesu alitukuzwa

"wakati Mungu alimtukuza Yesu"

walikumbuka ya kuwa mambo haya aliandikiwa yeye

Yohana, mwandishi, anafafanua hapa ili kumpa msomaji taarifa za jinsi mitume walivyoelewa baadaye.

John 12:17

ishara hii

Hili ni tukio au tokeo linalodhihirisha kuwa jambo fulani ni la kweli; kwa hali hii, inathibitika kuwa Yesu ni Masihi.

tazama, ulimwengu umekwenda kwake

"inaonekana kuwa kila mtu anakuwa mwanafunzi wake"

ulimwengu

neno hili limaanisha watu wote duniani

John 12:20

kisha baadhi ya Wayunani

hii inatoa utambulisho wa wahusika wapya katika simulizi

kuabudu katika sherehe

Yohana anamaanisha kuwa Wayunani walikuwa wanaenda kumwabudu Mungu wakati wa Pasaka.

Bethsaida

huu ulikuwa mji katika jimbo la Galilaya

na kisha wakamwambia Yesu

Filipo na Andrea wakamwambia Yesu kuhusiana na Wayunani walioomba kukutana naye.

John 12:23

Maelezo ya jumla:

Yesu anaanza kuwajibu Filipo na Andrea.

Amini, amini, nawaambia, chembe ya ngano isipoanguka katika nchi ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, itazaa matunda mengi.

"Kuwa makini zaidi na mfano huu ninaowaambia. Uhai wangu ni kama mbegu iliyopandwa katika nchi na kufa. Kama isipopandwa, hubakia mbegu moja tu. Lakini ikipandwa, hubadilika na kukua kwa kuzaa mbegu nyingi zaidi."

John 12:25

Yeye apendaye uhai wake ataupoteza; bali yeye auchukiaye uhai wake katika ulimwengu huu atausalimisha hata uzima wa milele.

"Kwa jinsi iyo hiyo, yeyote apendaye mapenzi yake, huyaharibu maisha yake. Bali yeye asiyefuata mapenzi yake, kwasababu ya utii kwangu, ataishi na Mungu milele."

anapenda maisha yake...huchukia maisha yake

Hii inamaanisha uzima wa mwili.

John 12:27

Niseme nini? Baba, niokoe mimi na saa hii?

Hii ni lugha ya balagha. Japokuwa Yesu anatamani kuepuka mateso, bado anachagua kumtii Mungu na kuuawa.

Baba

Hiki ni cheo cha muhimu cha Mungu

saa hii

Hii inamaanisha wakati Yesu atateswa na kufa msalabani.

ulitukuze jina lako

ufunue utukufu wako (Mungu) ili ujulikane

sauti ikaja kutoka mbinguni

Mungu aliongea kutoka mbinguni

John 12:30

Maelezo ya jumla

Yesu anaelezea sababu za sauti kutoka mbinguni

Sasa ni wakati wa hukumu ya ulimwengu

ulimwengu humaanisha watu wote walio duniani

sasa mtawala wa dunia hii atatupwa nje

mtawala wa dunia hii ni Shetani

John 12:32

Maelezo ya jumla:

Katika mstari wa 33 Yohana anaeleza historia ya maneno ya Yesu aliposema habari za kuinuliwa juu.

nitakapoinuliwa juu kutoka katika nchi

Hapa Yesu anamaanisha kusulubiwa kwake.

nitawavuta wote kwangu

Kwa kusulubiwa kwake, Yesu atafanya njia kwa ajili ya kila mmoja kumwamini yeye.

John 12:34

Mwana wa Mtu ni lazima atainuliwa juu

Neno "kuinuiwa juu" maana yake ni kusulubiwa.

Huyu mwana wa Mtu ni nani?

Maana yake ni, sifa za mwana wa mtu ni zipi?

John 12:37

Maelezo ya jumla:

Yohana anaanza kuongelea juu ya kutimizwa kwa unabii ambao nabii Isaya alitabiri.

ili kwamba neno la nabii Isaya litimizwe

kwa ajili ya kutimiza ujumbe wa nabii Isaya

mkono wa Bwana

Hii inamaanisha, uwezo wa Bwana wa kuokoa kwa nguvu.

John 12:39

ameifanya mioyo yao kuwa migumu

Huu ni msemo wenye maana kwamba Mungu amewafanya kuwa wasumbufu

mioyo yao kuelewa

Wayahudi waliamini kuwa moyo ndicho kiungo kinacholeta uelewa

John 12:41

ili kwamba wasifukuzwe katika Sinagogi

ili kwamba watu wasiwazuie kwenda kwenye Sinagogi

Walipenda sifa za wanadamu kuliko sifa zitokazo kwa Mungu

Walitaka watu wawasifie zaidi kuliko Mungu

John 12:44

Maelezo ya jumla

Huu ni wakati mwingine ambapo Yesu anaanza kuongea na makutano

Yesu alilia na kusema

Hii inamaanisha kuwa Yesu alipiga kelele na kusema

yeye anionaye mimi amemwona yule aliyenituma

"yeye" hapa inamaanisha "Mungu"

John 12:46

Sentensi unganishi:

Yesu anaendelea kuongea na makutano

Nimekuja kama nuru

Hii inamaana ya "Nikuja kuwaonesha iliyo kweli"

wasibaki gizani

"giza" hapa humaanisha kuishi katika ujinga wa kutokujua kweli ya Mungu.

John 12:48

katika siku ya mwisho

wakati ambapo Mungu atahukumu dhambi za watu

Nami najua ya kuwa amri yake ni uzima wa milele

Nami najua ya kuwa maneno aliyoniagiza mimi kusema ni maneno yaletayo uzima milele.

Baba

Hiki ni cheo cha muhimu cha Mungu

John 13

Yohana 13 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Matukio ya sura hii hujulikana kama chakula cha jioni la mwaisho au Meza ya Bwana. Sikukuu ya Pasaka kwa njia nyingi inafanana na dhabihu ya Yesu kama kondoo wa Mungu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#passover)

Dhana maalum katika sura hii

"Kuosha miguu ya wanafunzi"

Miguu ilioneka kuwa chafu sana katika inchi ya kale ya Mashariki ya Karibu. Ilikuwa ni kawaida mtumishi kuwa na jukumu la kuosha miguu ya bwana wake. Hatua hii ingechukuliwa kuwa cha aibu kwake Yesu, na ndiyo sababu wanafunzi hawakutaka afanye hivyo. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

Kuosha

Taswira ya kuosha hutumiwa hapa usiku wa kifo cha Yesu. Ni Yesu ambaye anaweza kuwasafisha watu. Taswira hii inawakilisha uwezo wa "kufanya haki." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#clean and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous).

Mimi ndimi

Yohana anatumia maneno haya mara saba katika injili yake. Ni maneno sawa yanayotumiwa na Mungu, alipojidhihirisha pamoja na jina lake Yahweh katika kichaka kilichokuwa kinawaka. Jina "Yahweh" linaweza kutafsiriwa kama "kama Mimi ndimi." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#reveal)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Mwana wa Binadamu"

Yesu anajiita mwenyewe kama "Mwana wa Binadamu." Lugha zingine haziwezi kuruhusu mtu kujitaja mwenyewe kama 'mtu wa tatu.'

<< | >>

John 13:1

Maelezo ya jumla

Kipindi hiki siyo cha Pasaka lakini tayari Yesu ameketi na wanafunzi wake mezani.

mpendwa

Hii ni aina ya upendo utokao kwa Mungu

Baba

Hiki ni cheo cha muhimu cha Mungu

John 13:3

Sentensi unganishi

Mstari wa 3 unaendelea kutufahamisha mambo ambayo Yesu aliyajua.

alivitoa vitu vyote kwa mkono wake

Hapa 'Mkono" unamaanisha mamlaka

alitoka kwa Mungu na alikuwa anarejea kwa Mungu

Yesu alikuwa na Baba siku zote, na angerudi kwake baada ya kumaliza kazi yake hapa duniani.

John 13:6

Bwana, unataka kuniosha miguu yangu?

Swali la Petro linaonesha kwamba hayupo tayari kuosha miguu yake na Yesu.

Kama sitakuosha miguu, basi hauna shirika nami

Yesu anatumia maneno magumu kumshawishi Petro akubali kuoshwa miguu.

John 13:10

Sentensi unganishi

Yesu anaendelea kuongea na Simoni Petro

Maelezo ya jumla:

Yesu anatumia neno "ninyi" kumaanisha wanafunzi wake wote.

John 13:12

Je mwajua nimefanya nini kwenu?

Yesu anajaribu kusisitiza mafundisho yake kwa wanafunzi wake

Ninyi mnaniita mimi 'mwallimu' na 'Bwana'

Yesu anamaanisha kuwa wanafunzi wake wanamheshimu sana.

John 13:16

Sentensi unganishi:

Yesu anaendelea kuongea na wanafunzi wake

mkubwa

wa muhimu zaidi

umebarikiwa

kubariki hapa kuna maana ya kusababisha vitu vizuri, vyenye faida kumpata mtu.

John 13:19

nawaambieni sasa kabla haijatokea

Ninawaambieni sasa yale yatakayotokea kabla hayajatokea

mpate kuamini kuwa MIMI NDIYE

mpate kuamini ya kuwa Mimi ndiye niliyesema kuwa Nipo

John 13:21

mwenye shida

nisiye na furaha

amini, amini

Tazama tafasiri katika 1:49

John 13:23

mmoja wa wanafunzi ambao Yesu alimpenda

Hii inamaanisha Yohana

kifua cha Yesu

kuweka kichwa kwenye kifua cha mwingine ilikuwa utamaduni mwingine wa Kiyunani uliomaanisha urafiki wa karibu

John 13:26

Iskarioti

Hii inamaanisha kuwa Yuda alitoka katika kijiji cha Keriothi

Shetani akamwingia

Hii inamaana kwamba Shetani alimteka na kumwongoza

John 13:28

kwamba awape maskini kitu

Unaweza kutafasiri hii kama, "Nenda na uwape maskini fedha"

aliondoka na kwenda haraka. Ilikuwa usiku

Yohana anamaanisha hapa kwamba Yuda angefanya uovu wake gizani wakati wa usiku

John 13:31

sasa mwana wa Mtu ametukuzwa na Mungu ametukuzwa ndani yake

Unaweza kutafasiri hii hivi, "Sasa watu wataona jinsi ambavyo mwana wa Mtu atapokea heshima na jinsi ambavyo Mungu atapokea heshimu kupitia yale anayoyafanya mwana wa Mtu."

watoto wadogo

Yesu anatumia neno watoto wadogo kumaanisha kwamba aliwapenda wanafunzi wake kama watoto wake.

kama nilivyosema kwa Wayahudi

Hii inamaanisha viongozi wa Kiyahudi

John 13:34

Sentensi unganishi:

Yesu anaendelea kuongea na wanafunzi wake

upendo

Hii ni aina ya upendo utokao kwa Mungu wenye kuleta mema kwa wengine

kila mtu

Hii ni hali ya kutia chumvi katika usemi kwamba kwa kila mtu aonaye upendo wa wanafunzi wake.

John 13:36

kuweka chini uhai wangu

kuutoa uhai wangu au kufa

Je utautoa uhai wako kwa ajili yangu?

Hii ni hali ya kuweka mkazo katika sentensi kwamba "wewe unasema utautoa uhai wako kwa ajili yangu..."

John 14

Yohana 14 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

"Nyumba ya Baba yangu"

Hii sio kurejelea hekalu. Lakini, ni kurejelea makao ya Mungu mbinguni. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#heaven)

Mfariji

Hili ni jina lingine la Roho Mtakatifu, pamoja na "Roho wa Kweli." Alikuwa tayari ulimwenguni, lakini angekuja kwa njia maalum, kukaa kati ya Wakristo, milele. Yesu na Roho Mtakatifu wote ni Mungu; kwa sababu ya ukweli huu, mtu anaweza kusema kwamba Yesu atakaa katika Wakristo baada ya kifo chake. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#holyspirit)

<< | >>

John 14:1

Usiruhusu moyo wako kuwa katika mahangaiko.

Huu ni msemo wenye maana kwamba , "acha kuogopa na kuwa na mashaka"

Katika nyumba ya Baba yangu kuna makazi mengi...

Mungu Baba ametayarisha eneo mbinguni kwa kila mtu ambaye ni muumini, kuishi pamoja naye na Mwanawe milele.

Baba

Hiki ni cheo cha muhimu kwa ajili ya Mungu.

John 14:4

Je! Twawezaje kuijua njia?

"Je! Tunawezaje kujua namna ya kufika pale?"

njia

Hii inaweza kuwa 1)"njia kwa Mungu" au 2) "mtu yule awapelekaye watu kwa Mungu."

kweli

Hii inaweza kuwa 2) "mtu wa kweli" au 2) "mtu anayenena maneno ya kweli."

uzima

"mtu ambaye anaweza kuwafanya watu wawe hai."

Yesu alimwambia, "Mimi ni njia, kweli, na uzima; hakuna mmoja wenu huja kwa Baba isipokuwa kupitia kwangu

Yesu, Mwana wa Mungu, ni njia pekee kwenda kwa Mungu Baba.

Baba

Hiki ni cheo muhimu kwa ajili ya Mungu.

John 14:8

Je! Sijakuwa pamoja nanyi kwa muda mrefu, na bado hunijui mimi, Philipo?

"Nimekuwa tayari pamoja nanyi wanafunzi kwa muda mrefu sana. Wewe, Philipo ungenijua mimi kwa wakati huu."

Jinsi gani unasema, 'Tuonyeshe Baba?

"hivyo wewe, Philipo, hakika usingekuwa unasema, 'Tuonyeshe Baba."

Bwana, tuonyeshe Baba...

Kumwona Mungu Mwana, Yesu, ni kumwona Mungu Baba.

John 14:10

Hamniamini mimi?

"Hakika mngeamini kuwa Baba yu ndani yangu."

Baba

Hiki ni cheo muhimu kwa ajili ya Mungu.

Maneno ninayoyasema kwenu sisemi kwa mamlaka yangu mwenyewe

"Ujumbe ninaowaambia hautokani na mawazo yangu mwenyewe."

Mimi ni ndani ya Baba, na Baba yangu yu ndani yangu

Kumwamini Yesu, Mwana wa Mungu, ni kuwamini Mungu Baba. Nafsi za Mungu ziko kwa kila yeyote kwasababu kila nafsi ya Mungu na zote katika Mungu, kupitia nafsi hizo zi tofauti kutoka kila moja.

John 14:12

amini, amini

Hii ina maana ya kumwamini Yesu, ndiyo kwamba, Kuamini kwamba ni Mwana wa Mungu, kumtumaini yeye kama Mwokozi, na kuishi katika njia ambayo inamweshimu yeye.

Chochote mkiombacho katika jina langu, nitafanya

Hii ni hali ya kuonesha ukuu na uwezo wa Yesu

Baba...Mwana

Hivi na vyeo muhimu vikielezea uhusiano kati ya Mungu na Yesu.

John 14:15

Mfariji

Neno linaelezea Roho Mtakatifu, "ambaye atakuja karibu kuwasaidia." Kuwafundisha wanafunzi

Roho wa Kweli

Roho Mtakatifu

ambaye ulimwengu hautampokea

Hapa neno "ulimwengu" linamaanisha watu wasioamini. Watu walio kinyume na Mungu.

John 14:18

Ulimwengu

Watu ambao hawajamwamini Mungu

mtajua kwamba mimi niko ndani ya Baba

Kuamini kwa kweli katika Kristo, Baba na Mwana huishi ndani ya muumini kupitia Roho.

Baba yangu

Hiki ni cheo muhimu kwa ajili ya Mungu

John 14:21

kupenda

Aina ya upendo huu huja kutoka kwa Mungu na unalenga kufanya mema kwa wengine, hata kama hautafaa kwa mhusika. Aina ya upendo huu hujari wengine, haijalishi wanafanya nini.

Yeyote anipendaye mimi atapendwa na Baba yangu

Wakati mmoja anampenda Yesu, naye Baba ampenda mtu yule.

Baba yangu

Hiki ni cheo muhimu kwa ajili ya Mungu.

Yuda (Siyo Iskarioti)

Huyu ni Yuda mwingine si yule aliyemsulubisha Yesu.

John 14:23

Sentensi unganishi:

Yesu anamjibu Yuda (Siyo Iskarioti)

Baba yangu

Hiki ni cheo muhimu kwa ajili ya Mungu

Neno ambalo mwasikia silo langu bali la Baba ambaye kanituma.

Yesu anasema kwamba yale ayasemayo yatoka kwa Baba. Ujumbe wa Yesu pia ni ujumbe wa Baba kwasababu Baba na Mwana wanakubaliana kikamilifu siku zote

Neno

Hii inaweza pia kuwa ujumbe

John 14:25

Mfariji

Roho Mtakatifu

Ulimwengu

Neno linaelezea watu wa ulimwengu huu.

Katika jina langu

Neno hapa "Jina" linaelezea juu ya nguvu na mamlaka ya Yesu

Baba

Hiki ni cheo muhimu cha Mungu.

John 14:28

Mpendwa

Aina ya upendo huu kutoka kwa Mungu unalenga kuwatendea mema wengine, hata wakati usipomfaidia mwenyewe. Upendo wa aina hii unajali wengine, bila kujali wanafanya nini.

Baba ni mkuu kuliko mimi

Mungu Baba ni mkuu kuliko Yesu, aliyekuwa akipitia kudharauliwa kama mwanadamu, lakini umilele, kama nafsi ya Mungu, wote wako sawa

Baba

Hiki ni cheo muhimu kwa ajili ya Mungu

John 15

Yohana 15 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Mzabibu

Mzabibu ni mfano muhimu katika maandiko. Sura hii inaunda mfano mgumu na uliopanuliwa. Masuala mbalimbali ya mfano huu na jinsi hutumiwa italetea watafsiraji magumu katika lugha zote. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

Mimi ndimi

Yohana anatumia maneno haya mara saba katika injili yake. Ni maneno sawa yanayotumiwa na Mungu, alipojidhihirisha pamoja na jina lake Yahweh katika kichaka kilichokuwa kinawaka. Jina "Yahweh" linaweza kutafsiriwa kama "Mimi ndim." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#reveal)

<< | >>

John 15:1

Sentensi unganishi

Simulizi inaendelea. Yesu anaketi mezani pamoja na wanafunzi wake

Mimi ni mzabibu wa kweli

Yesu anajilinganisha mwenyewe na mzabibu kwa kuwa yeye ni chanzo cha uzima.

Baba yangu ndiye mkulima

Hii inamaanisha "Mungu" ni kama mkulima

John 15:3

kaeni ndani yangu

endeleeni kukaa/kuungana na mimi, nami nitaendelea kukaa na ninyi.

mpaka mtakapokaa ndani yangu

Hii ni hali ya kundelea kumtegmea Yesu

Ninyi

Neno hili limetumika katika wingi

John 15:5

Mimi ni mzabibu, ninyi ni matawi

Mzabibu unamwakilisha Yesu. Matawi yanawakilisha wale wote wanaomwamini Yesu.

Yeye akaaye ndani yangu nami ndani yake

Yesu anajaribu kueleza kuwa wanafunzi wake wameunganisha na yeye kama yeye alivyounganishwa nao

huzaa sana

Hii inamwelezea muumini anayempendeza Mungu kwamba kama vile tawi lizaalo sana.

ombeni lolote mtakalo

Yesu anawaambia waumini kwamba ni lazima wamuombe Mungu ajibu maombi yao.

John 15:8

Baba yangu anatukuzwa katika hili

Unaweza kutafasiri hii kama, "Inawafanya watu wamuheshimu Baba yangu"

Baba yangu

Hiki ni cheo cha muhimu cha Mungu

ya kwamba mzae matunda mengi

hapa matunda yametumika badala ya maisha yanayompendeza Mungu

ni wanafunzi wangu

dhihirisheni ya kuwa mu wanafunzi wangu

dumuni katika pendo langu

endeleeni kupokea upendo wangu

John 15:10

Ikiwa mtazishika amri zangu, mtadumu katika pendo langu kama nilivyozshika amri za baba yangu na kudumu katika pendo lake.

Wanafunzi wanapomtii Yesu, wanaonesha upendo wao kwake.

Baba yangu

Hiki ni cheo cha muhimu cha Mungu

ili kwamba furaha yenu ifanyike kuwa timilifu

Unaweza kutafsiri hii kama, "ili furaha yenu itimie."

John 15:12

Hakuna mtu aliye na upendo mkuu kuliko huu

Upendo wa aina hii unatoka kwa Mungu na unawafaidia wengine pasipo kujali matendo yao.

Uhai

uzima wa kimwili

John 15:14

Ninyi ni rafiki zangu ikiwa mtafanya yale niwaagizayo

Mnaonesha ya kuwa mu rafiki zangu ikiwa mtaendelea kufanya yae niliyowaagiza

nimewajulisha mambo yote ambayo nimesikia kutoka kwa Baba

Nimewaambia kila kitu ambacho Baba yangu aliniambia.

Baba yangu

Hiki ni cheo muhimu cha Mungu

John 15:16

Hamkunichagua mimi

Yesu anasema kuwa wanafunzi wake hawakuchagua wenyewe kuwa wanafunzi

nendeni mkazae matunda

hii inamaanisha kuishi maisha yanayompendeza Mungu

kwamba matunda yenu yapate kukaa

matokeo ya matendo yenu yadumu milele

lolote muombalo kwa Baba kwa jina langu, atawapeni

"jina langu" ni kiwakilishi cha mamlaka ya yesu.

Mambo haya ninawaagiza, kwamba mpendane kila mtu na mwenzake

Upendo wa aina hii unatoka kwa Mungu na unawafaidia wengine pasipo kujali matendo yao.

John 15:18

kama ulimwengu utawachukia....

Yesu anatumia neno Ulimwengu kumaanisha watu ambao hawamwamini Mungu

upendo

Hii inarejea upendo wa kibinadamu, wa undungu, rafiki au mtu wa familia

John 15:20

Kumbukeni neno ambalo niliwaambia

Hii ni sawa na kusema kumbukeni ujumbe niliowaambia

kwa ajili ya jina langu

kwa sababu ni watu wangu

John 15:23

Yeye anichukiaye mimi humchukia Baba yangu pia ..... wameona na wamenichukia mimi na Baba yangu

Kumchukia Mungu mwana ni kumchukia Mungu Baba pia.

wangelikuwa hawana dhambi

wasingekuwa wamefanya dhambi

sheria

Hii inamaanisha Agano la Kale lote ambalo lilikuwa na maagizo yote ya Mungu kwa wanadamu

John 15:26

Mfariji

Hii inamaanisha Roho Mtakatifu

Roho wa Kweli

Roho ambaye atawaambia kweli yote

Ninyi pia mnashuhudia

Kushuhudia ni kuwaambia wengine habari za Yesu

Mwanzo

Hii inamaanisha siku za mwanzo za huduma ya Yesu.

John 16

Yohana 16 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Mfariji

Hili ni jina lingine la Roho Mtakatifu, pamoja na "Roho wa Kweli." Alikuwa tayari ulimwenguni, lakini angekuja kwa njia maalum, kukaa kati ya Wakristo, milele. Yesu na Roho Mtakatifu wote ni Mungu; kwa sababu ya ukweli huu, inaweza kusemekana kwamba Yesu atakaa katika Wakristo baada ya kifo chake. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#holyspirit)

"Saa inakuja"

Haya ni maneno ambayo yanaweza pia kutafsiriwa kama "wakati unakuja." Yesu anaelezea wakati baada ya kifo chake kama saa hii itakapokuja. Ukitumia maneno haya, yataweza kuonekana kama unabii. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#prophet)

Mifano muhimu za usemi katika sura hii

Mfan

Yesu analinganisha kifo chake na maumivu ya mwanamke anayezaa. Ni kwa maumivu ambapo maisha mapya huja. wakati wa mfano huu kusemwa, hakuna hakika ya wasikilizaji kuelewa mfano huu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

<< | >>

John 16:1

Sentensi unganishi:

Yesu ameketi chakulani na wanafunzi wake na anaendelea kuwafundisha

hamtaanguka

Hii inamaanisha kuwa hamtaiacha imani ndani ya Yesu.

John 16:3

Watawatendea haya kwa sababu hawamfahamu Baba wala mimi.

Baadhi ya waamini wanaweza kuuawa kwa sababu wasiomjua Mungu Baba pia hawamjui wala kumuelewa Mungu Mwana, Yesu Kristo.

Baba

Hiki ni cheo cha Muhimu cha Mungu.

Hapo mwanzo

Angalia ulivyotafsiri "tangu mwanzo" kwenye Yohana 15:26

John 16:5

Kama nisipoondoka, mfariji hatakuja

"Mfariji atakuja ikiwa nitaondoka"

Mfariji

Angalia jinsi ulivyotafsiri kwenye Yohana 14:25

John 16:8

Mfariji atauhukumu ulimwengu kutokana...haki...naenda kwa Baba

Yesu alipoondoka duniani na akarudi kwa Mungu Baba, kisha Mungu Roho akaanza kuwaonyesha watu wana dhambi na wanahitaji msamaha unaopatokana kwa Yesu pekee.

Ulimwengu

Inamaanisha watu wanaoishi duniani

kutokana na haki, kwa sababu naenda kwa Baba, na hamtaniona tena

"Atawaambia watu kwamba kwa sababu narudi kwa Baba, hamtaniona tena, mtajua kuwa ni mimi mwenye haki ya kweli"

Baba

Hiki ni cheo cha muhimu cha Mungu.

Mkuu wa ulimwengu

Angalia jinsi ulivyotafsiri kwenye Yohana 12:30

John 16:12

Mambo ya kuwaambia

"ujumbe kwa ajili yenu"

Roho wa kweli

Hili ni jina la Roho Mtakatifu atakayewaambia watu kweli ya Mungu

atawaongoza katika kweli yote

kweli inamaanisha ukweli wa kiroho

John 16:15

Vitu vyote...alivyonavyo Baba ni vyangu...Roho atachukua mambo yangu

Mungu Baba, Mwana, na Roho wote wanamiliki ulimwengu. Kwa pamoja ni wamoja na ni Mungu pekee.

Baba

Hiki ni cheo muhimu cha Mungu.

Muda mfupi

"karibu" au "kabla ya muda mrefu"

John 16:17

Maelezo ya jumla:

Wanafunzi wanaulizana kuhusu alichosemaYesu

muda mfupi na hamtaniona tena

wanafunzi hawakuelewa kuwa yesu alikuwa anaongelea kifo chake msalabani

na kisha muda mfupi mtaniona

Hii inaweza kumaanisha kufufuka kwa Yesu, au kuja kwa Yesu mara ya pili

Baba

Hiki ni cheo muhimu cha Mungu

John 16:19

Sentensi unganishi:

Yesu anaendelea kuongea na wanafunzi wake

amini, amini nawaambia

tafsiri kwa kuonesha kuwa kifuatacho ni cha muhimu zaidi

lakini ulimwengu utashangilia

lakini watu wanaompinga Mungu watashangilia

John 16:22

Kama mkiomba lolote kwa Baba, atawapa kwa jina langu

Baba na Mwana wanajibu maombi pamoja. Wanaomwamini Yesu wana msamaha wa milele wa dhambi na wanaweza kuomba kwa Baba kupitia kwa Mwana, na Baba atajibu.

Baba

Hiki ni cheo cha Muhimu cha Mungu.

Kwa jina langu

Baba atawapatia mahitaji yao kwa sababu ya mahusiano yao na Yesu. "kwa sababu ni wafuasi wangu" au "kwenye mamlaka yangu"

John 16:25

Kwa lugha isiyoeleweka

"kwa lugha ambayo ni ngumu kueleweka"

Nitawaambia waziwazi kuhusu Baba

Kibinadamu kujifunza kuhusu Mungu Baba kupitia Mwana wa Mungu, Yesu. Kumjua Mwana ni kumjua Baba.

Baba

Hiki ni cheo muhimu cha Mungu.

John 16:26

Baba mwenyewe anawapenda kwa sababu mmenipenda mimi

Mtu akimpenda Yesu, Mwana, pia anampenda baba, kwa sababu Baba na Mwana ni mmoja.

Baba

Hiki ni cheo muhimu cha Mungu.

Nilitoka kwa Baba... Naondoka ulimwenguni na ninaenda kwa Baba.

Baba alimtuma mwana msalabani awaokoe waamini toka kwenye dhambi na jehanamu, akafufuka toka kwa wafu, na akarudi Mbinguni.

Ulimwengu

"dunia." Ni mahali ambapo watu wanaishi.

John 16:29

Sentensi unganishi:

wanafunzi wanamjibu Yesu

Sasa mmeamini?

"Hatimaye sasa mmeiweka imani yenu kwangu!"

John 16:32

Sentensi unganishi:

Yesu anaendelea kuongea na wanafunzi wake

nanyi mtatawanyika

"wengine watawatawanya"

Baba yu pamoja nami

Hili jina la muhimu la Mungu

ili kwama ndani yangu muwe na amani

amani ya ndani

nimeushinda ulimwengu

nimezishinda taabu na mateso ya duniani

John 17

Yohana 17 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Sura hii ni sala moja ndefu.

Dhana maalum katika sura hii

Yesu ni wa milele

Sura hii inaonyesha wazi kwamba Yesu alikuwepo kabla ya ulimwengu kuumbwa.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Sala

Sala inaweza kuwa dhana ngumu kutafsiri katika tamaduni ambazo hazijui desturi hii. Kwa kuwa Yesu ni Mungu, sala zake si kama sala za watu wengine. Sura hii inaweza kuwa vigumu sana kuelewa kwa sababu Yesu hakuhitaji kuomba msaada, na sala zake pia zinaweza kuonekana kama amri. Haingekubalika kwa mtu mwingine kuomba kwa namna hii.

<< | >>

John 17:1

Baba ...mtukuze mwanao ili na mwana naye akutukuze wewe

Yesu anamwomba baba yake, Mungu Baba amtukuze, mwana wa Mungu

Baba...Mwana

Hivi ni vyeo vya mhimu amabavyo huelezea uhusiano kati ya Mungu na Yesu

Mbingu

Hii inamaanisha sehemu ya juu

John 17:3

Na uzima wa milelel ndio huu...wakujue wewe Mungu wa kweli, na.. Yesu Kristo

Uzima wa milele ni kumjua Mungu wa kweli na wa pekee, Mungu Baba na Mungu Mwana na Mungu Roho.

Kwamba inawapasa wakujue wewe

Hii inamaanisha kumjua mungu kwa uzoefu na wala si juu ya Mungu

Ile kazi uliyonipa kuifanya

"Kazi"inamaanisha jumla ya huduma ya Yesu hapa Duniani.

Baba, nitukuze mimi...kwa niliokuwa nao nilipokuwa na wewe kabla dunia haijaumbwa

Yesu alikuwa na utukufu pamoja na Mungu Baba '"Kabla ulimwengu haujaumbwa" Kwa sababu Yesu ni Mungu Mwana. Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu ndio Mungu wa Kweli ambaye amekuwepo milele yote na ataendelea kuwepo milele ne milele.

Baba...Mwana

Hivi ni vyeo vinavyoonyesha uhusiano kati ya Mungu na Yesu.

John 17:6

Si wa Dunia

Hapa neno "Dunia" humanisha watu wa dunia. Hii inamaanisha Mungu amewatofautisha na wale wasioamini.

Wamelishika neno lako

Wameyatii mafundisho yako

John 17:9

Mimi siuombei ulimwengu

Hapa neno ulimwengu linamanisha watu waovu duniani au watu wasiomtii Mungu

Duniani

Hii inamaanisha hali ya kuwa duniani na kuwa mmoja wa wale wanaoishi humo.

Baba Mtakatifu, uwalinde... ii wawe na umoja kama sisi tulivyo na umoja

Yesu anamwomba Baba ili awalinde wale wanaoamini. Mungu Baba huwalinda wale wanaomwamini Mungu Mwana na kuwafanya wawe na umoja na Mungu katika utatu wake

Baba

Hiki ni cheo muhimu cha Mungu

Uwalinde kwa jina lako ulilonipa mimi

Hapa neno "jina"linamaanisha ulinzi na usimamaizi wa Mungu. "Uwalinde na kwa ulinzi wa jina lako kama ulivyonilinda mimi" au "uwalinde kwa nguvu za jina lako ulilonipa mimi

John 17:12

Hakuna hata mmoja wao aliyepotea, isipokuwa mwana wa upotevu

"mtu pekee aliyepotea ni mwana wa upotevu"

mwana wa upotevu

"yule ambaye tokea awali uliamua kumwamngamiza"

ili kwamba maandiko yatimie

"Ili mambo yaliyoandikwa kwenye maandiko"

John 17:15

ulimwengu

watu wakaao duniani

uwalinde na yule mwovu

uwalinde didi a Shetani

uwaweke wakfu kwako katika kweli

wafanye kuwa watu wako kwa kuwafundisha kweli

Neno lako ndiyo kweli

ujumbe wako ni kweli au unachosema ni kweli

John 17:18

ulimwenguni

kwa kila mtu duniani kote

ili kwamba na wao wajitoe kwako kwa ile kweli

unaweza pia kutafsiri kuwa: "ili kwamba wajitoe kikamilifu kwako"

John 17:20

ili kwamba wote wawe na umoja...kama, vile wewe Baba, ulivyo ndani yangu, na mimi ndani yako...ili kwwamba wao pia wawezekuwa ndani yetu

Mungu Baba yumo ndani ya Mungu Mwana na mwanaYumo ndani ya Baba. Wla wamwaminioa Yesu, Mungu mwana huwa na umoja na Baba na mwana wamwaminipo.

Baba

Hiki ni cheo muhimu cha Mungu

Dunia

Hii humanisha watu wa duniani

John 17:22

Utukufu ule ulionipa mimi nimewapa wao

nimewaheshimu wafuasi wangu kama ambavyo wewe umeniheshimu mimi

ili kwamba waweze kuwa na umoja

Unaweza kutafsiri kama: "ili uweze kuwaunganisha kama ambavyo umetuunganisha sisi"

kukamilishwa katika umoja

kuwa kitu kimoja

ili ulimwengu ujue

ulimwengu ni watu

John 17:24

Baba...ulinipenda mimi kabla y kuumbwa kwa isingi ya ulimwengu

Mungu Baba amempenda Mungu mwana. Kabla Mungu hajauumba ulimwengu, nafsi za Mungu hupendana, na zitaendelea kupendana milele yote.

Nilipo mimi

hii inamaanisha mbinguni

ili waweze kuona utukufu wangu

ili waweze kujua ukuu wangu

kabla ya kuumbwa kwa ulimwengu

Hapa Yesu anamaanisha wakati wa kabla ya uumbaji

John 17:25

Ulimwengu haukukutambua, lakini mimi nakujua; na hawa wanajua kuwa ulinituma

"ulimwengu hauna uzoefu wa kukujua wewe kama ninavyokujua; na hawa wanajua kuwa wewe umenituma"

jina

Hili linamanisha Mungu.

lile pendo...ulilonipenda

Upendo wa jinsi hii hutoka kwa Mungu na hulenga mema ya wengine, hata kama hauna maslahi binafsi. Upendo wa jinsi hii huwajali wengine bila kujali wanachofanya

Mungu mwenye haki

Hiki ni cheo cha muhimucha Mungu

John 18

Yohana 18 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Mistari ya 13 na 14 inasema, "kwa kuwa alikuwa baba mkwe Kayafa, ambaye alikuwa kuhani mkuu mwaka huo. Sasa Kayafa ndiye aliyewapa Wayahudi ushauri kwamba ingekuwa bora kwamba mtu mmoja afe kwa ajili ya watu . " Hii ni taarifa ya mabano inayotolewa na mwandishi. Inalenga kuelezea taarifa muhimu ya historia. Inawezekana kuweka taarifa hii kwa mabano.

Dhana maalum katika sura hii

"Sio halali kwetu kumwua mtu yeyote"

Ufalme wa Kirumi haukuruhusu Wayahudi kutekeleza adhabu ya kifo kwa mtu yeyote. Kwa hiyo, Wayahudi walipaswa kuwasilisha kesi yao kwa mtawala wa kipagani, Pilato.

Ufalme wa Yesu

Yesu anamwelezea Pilato kwamba ufalme wake sio "wa ulimwengu huu." Wataalamu wengine huchukua hii kumaanisha ya kwamba Yesu anatawala ufalme wa kiroho, lakini wengine wanasema kama maana ya maneno ya Yesu ilikuwa kama ufalme wake haukushindana na ufalme wa Kirumi. Inawezekana kutafsiri maneno haya kama ufalme wa Yesu "haukuanzisha mahali hapa au huanzisha mahali pengine."

Mifano muhimu ya usemi katika sura hii

"Mfalme wa Wayahudi"

Maneno haya hutumiwa kwa njia mbili tofauti katika kifungu hiki. Kwanza, Yesu anasemekana kuwa mfalme wa Wayahudi. Yeye ndiye mfalme wa Wayahudi na ulimwengu wote. Pili, hutumiwa kwa kinaya au kudhihaki na Pilato. Pilato hakumwamini Yesu kuwa mfalme wa Wayahudi. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-irony)

<< | >>

John 18:1

Bonde la Kidron

Hili ni bonde liliko Yerusalem ambalo hutenganisha Mlima wa hekalu na Mlima wa mizeituni

palipokuwaa na bustani

hili lilikuwa shamba la mizabibu

John 18:4

Maelezo ya jumla:

Yesu anaanza kuongea na askari, waheshimiwa, na Mafarisayo

Naye Yesu hali akijua kila kitu kilichokuwa kikifanyika dhidi yake

Yesu alijua mambo yote yaliyopaswa kumpata

John 18:6

Mimi

Hapa neno "yeye" halipo kwenye tafsiri ya asili lakini limefananishwa tu na "mimi ndiye"

kuanguka chini

watu walianguka chini kwa sababu ya nguvu za Yesu

Yesu Mnazareth

Yesu, mtu wa kutoka Nazareth

John 18:8

Mimi ndiye

Hapa neno "yeye" halipo kwenye tasfsiri ya asili lakini limehusishwa tu.

Haya yalikuwa hivyo ili lile neno linalosema

"Neno" linamaanisha maneno ambayo Yesu aliyaomba.

John 18:10

Markusi

Markusi ni mtumishi wa kiume wa Kuhani Mkuu

Ala

Huu ni mkoba wakisu au sime unauzuia kisu kisimkate mwenye nacho

Kikombe

Hii inamaanisha 1) Kiasi cha mateso ambayo Yesu alitakiwa kuyapokea 2) Gadhabu ya Mungu ambayo Yesu ilimlazimu kuivumilia ili kuwalkomboa watu wake.

Je nisikinywee kikombe ambacho Baba yangu amenipa?

Yesu anahoji hili swali kuonesha msisitizo kwamba lazima ateseke.

Baba

Hiki ni cheo muhimu cha Mungu.

John 18:12

Maelezo ya jumla:

Mstari wa 14 unatoa maelezo yanayomhusu Kayafa

Wayahudi

hii inamaanisha viongozi wa Wayahudi

Walimkamata Yesu na kumfunga

Askari walimfunga Yesu mikono ili asitoroke

John 18:15

mwanafunzi mwingine, na yule mwanafunzi

Huyu ni mtume Yohana, mwandishi wa wa hii injili

John 18:17

Je, wewe si mmoja wa wanafunzi wa huyu mtu?

"Wewe ni mmoja wa wanafunzi wa huyu mtu"

John 18:19

Kuhani mkuu

Huyu alikuwa Kayafa

Nimeumbia waziwazi ulimwengu

Yesu aliifanya huduma yake katika uma wa watu

Hawa watu

Hawa ni wale watu waliomsikia Yesu akifundisha

John 18:22

Je, hivyo ndivo inavyokupas kumjibu kuhani mkuu?

'Hivyo sivyo inavyokupasa kumjibu Kuhani Mkuu"

uwe shahidi kwa ajili ya uovu

"niambie makosa yangu niliyoyasema"

kama nimejibu vyema kwa nini kunipiga?

"kama nimejibu kwa ukweli usinipige"

John 18:25

Maelezo ya jumla:

Hapa habari inarudi kumwelezea Petro.

Je, wewe ni mmoja wa wanafunzi wake?

Swali hili linatoa msisitizo wa ukweli wa jambo

Je si wewe niliyekuona naye kule bustanini?

hapa neno "naye" linamaanisha Yesu

Kisha Petro akamkana tena

Hii inamaanisha kuwa petro alimkana kwa kujua kuwa alikuwa na Yesu.

na papo kwa papo jogoo akawika

Ikumbukwe kuwa Yesu alimwambia Petro kuwa jogoo atawika kabla hajamkana

John 18:28

Maelezo ya jumla:

Askari na washitaki wa yesu wanamleta kwa Kayafa. Mstari wa 28 unaeleza sababu zilizowafanya wasiingie katika Praitorio.

Kama huyu mtu asingekuwa mtenda maovu, tusingemleta kwako.

Huyu mtu ni mtenda maovu, na ni lazima tumlete kwako ili aadhibiwe"

Kumleta

Hili neno "kumleta" linamaanisha kumkabidhi kwa adui

John 18:31

Maelezo ya jumla:

Kwenye mstari wa 32 mwandishi anaelezea jinsi ambavyo yesu alitabiri kifo chake

Wayahudi wakamwambia

Hawa ni viongozi wa Wayahudi aliompinga Yesu na kumkamata.

sheria haituruhusu sisi kumpa tu adhabu ya kifo

Kulingana na sheria ya Kirumi, Wayahudi wasingweza kumuua mtu.

John 18:33

Mimi siyo Myahudi, au sivyo?

Hapa Pilato anauliza swali kuelezea jinsi ambavyo hana haja na tamaduni za Kiyahudi

watu wako mwenyewe

Wayahudi wenzako

John 18:36

Ufalme wangu si wa ulimwengu huu

Sentesihii yaweza kumaanisha 1) "Ufalme wangu si sehemu ya dunia hii" au 2) "Si hitaji ruhusa ya dunia hii kuwa mtawala wao" au "Si kwa kutokana na ulimwengu huu kwamba nina mamalaka ya kuwa mfalme."

Ili kwamba nisitolewe kwa Wayahudi.

"wangewazuia viongozi wa Kiyahudi kunikamata"

Sauti yangu

"mambo ninayoyaongelea" au "mimi"

John 18:38

kweli ni nini?

"Hakuna awezaye kujua kitu kilicho cha kweli"

Wayahudi

hii inamaanisha viongozi wa Kiyahudi

siyo huyu, ufungulie Baraba

tafsri kuonesha kuwa hawakumtaka Baraba bali Yesu

Baraba alikuwa mnyang'anyi

Hapa Yohana anaeleza Baraba alikuwa mtu wa aina gani

John 19

Yohana 19 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri hupendelea kuweka nukuu za Agano la Kale. ULB na tafsiri nyingine nyingi za Kiingereza huingiza mistari ya 19:24, ambayo ni nukuu kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

"Vazi la zambarau"

Rangi ya zambarau ilikuwa ishara ya kifalme Rangi ya zambarau ilikuwa ishara ya kifalme katika Mashariki ya Karibu. Yesu alivikwa kuoneka kama mfalme kwa kumdhihaki. Yesu alikuwa amevaa kuonekana kama mfalme kwa kukejeliwa.

"Wewe si rafiki ya Kaisari"

Pilato hakutaka kumhukumu Yesu kwa kifo, lakini Wayahudi walimlazimisha. Walifanya hivyo ili kuifanya kuonekana kama kuruhusu Yesu kuishi kungeweza kusaliti serikali ya Kirumi.

Mifano muhimu ya usemi katika sura hii

Kudhihaki

Maneno yanayofuata yanatakiwa kuchukuliwa kudhihaki: "Salamu, Mfalme wa Wayahudi," "Je, nimsulubishe mfalme wenu?" na "Yesu wa Nazareti, Mfalme wa Wayahudi." Kudhihaki ni matumizi ya kinaya kumtukana mtu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-irony)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Gabbatha, Golgotha

Haya ni maneno mawili ya Kiebrania. Baada ya kutafsiri maana ya maneno haya ("Sakafu ya mawe" na "Mahali pa Fuvu"), mwandishi hufasiri sauti zao kwa kuandika kwa herufi za Kigiriki.

<< | >>

John 19:1

Salaam, mfalme wa Wayahudi

Hii "Salaam" inayoambatana na mkono ulioinuliwa ilitumika kwa msalimia Kaisari pekee yake. Wakati asakari wakitumia kofia ya miiba na vazi la dhambarau kwa kumkejeli Yesu, hawakumtambua kwa hakika kuwa ni mfalme.

John 19:4

Mimi sioni hatia yoyote ndani yake

Hii ni sawa na kusema kuwa sioni sababu ya kumwadhibu

taji ya miiba...vazi la dhambarau

taji na vazi la dhambarau ni vitu vinavyovaliwa na wafalme tu.

John 19:7

inampasa kufa kwa sababu yeye alijifanya kuwa mwana wa Mungu

Yesu alihukumiwa kufa kwa kifo cha kusulibiwa kwa sababu ya kudai kuwa yeye alikuwa "mwana wa Mungu"

Mwana wa Mungu

Hiki ni cheo cha muhimu cha Yesu

Wewe uatoka wapi?

"Unatoka wapi? Pilato alimuliza Yesu kwa ajili ya kujua utambulisho wake. utamaduni wako unaweza kuwa njia maalumu ya kutambua utamaduni wa mtu.

John 19:10

Je, wewe huongei na mimi?

Pilato anaonyesha kushangazwa na Yesu kwa kutokuitumia nafasi hiyo ya kujiteteta. "Nijibu"

Usingekuwa na nguvu kama usingepewa toka juu

"Una mamalaka kinyume changu kwa sababu tu umepewa"

aliyenitoa

Neno "kutoa" linamaanisha kumkabidhi Yesu kwa adui, kama vile Yuda alivyomtoa Yesu kwa viongozi wa Kiyahudi

John 19:12

ajaifanyaye kuwa mfalme

"madai ya kuwa yeye ni mfalme"

akamleta Yesu nje

Hii inamaanisha kuwa aliwaagiza askari kumleta Yesu nje il ikumwonyesha kwa makutano.

akakaa

Watu wakubwa walikaa wakati watu wengine amabao si wskubwa walisimama.

Kwenye kiti cha hukumu

Hiki ni kiti maalumu ambacho watu mhimu walikaa wakati wa kufanya maamuzi ya kiofisi. Utamaduni wako unaweza kuwa na njia tofauti wautaratibu huu.

Fuvu la kichwa

Hili ni eneo maalumu ambalo watu maalumu ndio wsalioruhusiwa kupaingia, Utamaduni wako unaweza kuwa na maeneo maalumu kama hili.

Kihebrania

Hii ilikuwa lugha ambayo wahebrania waliongea

John 19:14

Sentensi unganishi:

Muda umepita na sasa ni saa la sita, wakati Pilato anawaagiza askari wamsulibishe Yesu.

saa la sita

kama muda wa mchana

Pilato akwaambia Wayahudi

Hapa inamaanisha Pilato aliwaambia viongozi wa Kiyahudi

Je, mimi nimsulibishe mfalme wenu?

Pilato anawauliza Wayahudi ikiwa wanataka askari wake wamsulibishe Yesu.

John 19:17

kwenye eneo liitwalo fuvu la kichwa

Unaweza kutafsiri kama: "kwenye eneo ambalo watu wanaliita fuvu la kichwa"

ambalo kwa Kiebrania huitwa "Golgotha"

Kiebrania ni lugha ya Waisraeli

pamoja naye wanaume wawili

Unaweza kutafsiri kama: "pia waliwasulibisha wahalifu wengine wawili kwenye misalaba yao"

John 19:19

Pilato pia aliandika alama na kuiweka juu ya msalaba

hapa inamaanisha mtu aliyeandika kwa niaba ya Pilato na kuiweka juu ya msalaba wa Yesu

Hapo paliandikwa: YESU MNAZARETHH, MFALME WA WAYAHUDI

Unaweza pia kutafsiri hii kama: "hivyo yule mtu aliandika maneno haya: Yesu ya nazarethi, mfalme wa Wayahudi"

Kiyunani

Hii ni lugha ya serikali ya Kirumi

John 19:21

Kisha wakuu wa makuhani wa Wayahudi wakamwambia Pilato

Wakuu wa makuhani walienda mpaka Ikulu kumshitaki Yesu juu ya maneno na miujiza yake.

Niliyoyaandika nimeandika

Pilato anamaanisha kuwa hawezi kubadilisha maneno katika kibao

John 19:23

Maelezo ya jumla:

Mwishoni mwa mstari wa 24 kuna tofauti kutoka habari kwa kuwa Yohana anaelezea jinsi tukio hili linatimiza maandiko.

kanzu

askari waliweka kando kanzu na hawakuigawa

wakapiga kura

hivi ndivyo askari walivyogawana mavazi ya Yesu.

John 19:25

Yule mwanafunzi aliyempenda

Huyu ni Yohana mwandishi wa injili hii

Mwanamke, mtazame, mwanao huyu hapa

"Mwanamke, tazama na ufifkiri juu huyu mtu kama angekuwa mwano"

Mama yako huyu hapa

"fikiri juu ya huyu mwanamke kama angekuwa mama yako"

John 19:28

Siki

Hiki ni kinywaji cha makomamanga kilchokuwa kimechachushwa kwa muda mrefu

wakaweka

"Hawa" nia walinzi wa Kirumi

Sifongo

Hi ni kiufito kilichokuwa na uwezo wa kunyonya kimiminika

Akaisalimu roho yake

Yesu aliito roho yake kwa Mungu na kuruhusu mwili wake kufa

John 19:31

Wayahudi

Hii inamaanisha viongozi wa Kiyahudi

siku ya maandalio

Huu ni muda uliokuwa kabla ya pasaka ambao ulitumika kuandaa chakula

kuvunja miguu yao na kuiondoa

Unaweza kutafsiri kama, "kuvunja miguu ya waliosulibiwa na kuiondoa miili yao kutoka kwenye misalaba yao"

aliyekuwa amesulibiwa pamoja na Yesu.

Unaweza kutafsiri kama, "ambaye walimsulibisha karibu na Yesu"

John 19:34

Naye aliyeona hili

Sentesi hii inatoa mukhutadha wa habari. Mwandishi ambaye ni (Mtume Yohana) anawafahamisha wasomaji kuwa yeye alikuwepo na kwamba tukiamini alichoandika

John 19:36

Hapana mfupa wake utakaovunjwa

"Hakuna atayevunja hata mmoja ya mifupa yake"

John 19:38

Yusuph wa Arimathaya

Yusuph kutoka mji wa Arimathaya

kwa kuwaogopa wayahudi

"Kwa kuwahofia viongozi wa Kiyahudi"

Nikodemo

Huyu ndiye aliyeenda kwa Yesu wakati wa giza

manemane na udi

Haya ni manukato yaliyo kabla ya mazishitumika kuandaa maiti

Mia moja

Kipimo cha mia moja

Ratli

"Ratli moja" ni sawa na kipimo cha gramu 31

John 19:40

Sasa mahali ambapo Yesu alisulibiwa kulikuwa na bustani....hakuna mtu alikuwa amezikwa humo

Hapa mwandishi Yohana anatoa maelezo kuhusu mahali ambapo kaburi lilikuwa

Kwa sababu ilikuwa siku ya maandalio kwa Wayahudi

Kulingana na sheria ya Kiyahudi, hakuna mtu aliyeruhusiwa kufanya kazi baada ya jua kuzama. Ilikuwa ni mwanzo wa Sabato na Pasaka

John 20

Yohana 20 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

"Pokea Roho Mtakatifu"

Wanafunzi walikuwa na nguvu maalum waliopewa na Roho Mtakatifu. Aliiwezesha huduma yao.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Raboni

Hii ni neno la Kiebrania. Yohana "alifasiri" sauti zake kwa kubadilisha herufi za Kiebrania na kutumia herufi za Kigiriki. Kisha anaeleza kwamba maana ya neno hili ni Mwalimu." Mtafsiri anatakiwa kufanya hivyo, lakini aifasiri kwa kutumia herufi za lugha inayolengwa.

Mwili wa Yesu wa ufufuo

Kuna siri juu ya mwili wa Yesu wakati huu. Alikuwa kimwili mwenye makovu kutoka kusulubiwa lakini pia aliweza kuingia katika vyumba bila kutumia mlango. Ni vyema kuiacha hii siri mahali pale lakini maelezo yanaweza kuwa muhimu ikiwa tafsiri haieleweki kwa msomaji.

Malaika wawili wenye mavazi meupe

Mathayo, Marko, Luka, na Yohana wote waliandika juu ya malaika waliovalia nguo nyeupe wakiwa pamoja na wanawake katika kaburi la Yesu. Waandishi wawili kati yao waliwaita wanaume, lakini ni kwa sababu tu malaika walikuwa katika hali ya kibinadamu. Waandishi wawili waliandika kuhusu malaika wawili, lakini waandishi wengine wawili waliandika juu ya moja tu. Ni bora kutafsiri kila moja ya vifungu hivi kama inavyoonekana katika ULB bila kujaribu kufanya vifungu vyote kufanana.(Angalia: Mathayo 28: 1-2, Marko 16: 5 na Luka 24: 4 na Yohana 20:12)

<< | >>

John 20:1

Siku ya kwanza ya Juma

Jumapili

Mwanfunzi ambaye Yesualimpenda

Sentesi hii inaonekana kuwa ni njia ambayo Yohana aliitumia kumwonyesha yeye katika kitibu chote. Neno "upendo" linamaanisha upendo wa ndugu au upendo wa rafiki au kwa mwanafamilia

Wamemchukua

Mtu amechukua

John 20:3

mwanafunzi mwingine

Yohana anatumia neno hili kwa kuonyesha unyenyekevu akimaanisha yeye mwenyewe badala ya kutumia jina lake.

Sanda za kitani

Hizi zilikuwa nguo za mazishi zilizotumika kuuzongazonga mwili wa Yesu.

John 20:6

Sanda za Kitani

Hizi ni nguo azazovalishwa mfu kabla ya kuzikwa

leso ilyokuwa kichwani mwake

Hiki ni kitambaa kidogo ambacho hutumika kwa kufutia jasho usoni amabcho pia kilitumika kufunika uso wake

John 20:8

mwanafunzi mwingine

Yohana anatumia neno hili kwa kuonesha unyenyekevu akimaanisha yeye mwenyewe pasipo kutaja jina lake.

aliona na kuamini

Alipoona kuwa kaburi lipo wazi, aliamini ya kuwa yesu alikuwa amefufuka kutoka wafu

bado hawakuyajua maandiko

hapa mwandishi anawaongelea wanafunzi ambao hawakujua bado maandiko yanayosema kuwa Yesu angefufuka tena.

John 20:11

aliwaona malaika wawili na nguo nyeupe

Malaika walikuwa wamevaa nguo nyeupe

wakamwambia

walimuuliza

Kwa sababu wamemchukua Bwana wangu

Kwa sababu wameuchukua mwili wa Bwana wangu

Nami sijui walikomweka

Nami sijui walipouweka mwili

John 20:14

Yesu alimwambia

Yesu alimuuliza

Bwana, kama ni wewe uliyemchukua yeye

neno "yeye" hapa linarejjea kwa yesu

niambiie ulikomweka

niambie ulipokiweka

nami nitamchukua

Maria Magdalena anataka kuchukua mwili wa Yesu na kuuzika tena.

John 20:16

Rabboni

Neno "Rabboni" linamanisha rabi au mwalimu katika Matamushi ya Kiaramaic ya Mariamu

ndugu

Yesu alitumia neno "ndugu" akimaanisha wanafunzi wake

nitapaa kwenda kwa baba amabye pia ni baba yenu, Mungu wangu na Mungu wenu.

Yesu alifufuka toka wafu kisha akatabiri kupaa mbinguni, akirudi kwa Baba, Mungu Baba

Baba yangu na Baba yenu

Hivi ni vyeo muhimu vinavyofafanua uhusiano kati ya Yesu na Mungu, na kati ya waumini na Mungu.

John 20:19

Siku hiyo, siku ya kwanza ya juma

hii inamaanisha Jumapili

Amani iwe kwenu

hii ni salamu ya kawaida"

akawaonyesha mikono yake na ubavu wake

"aliwaonyesha vle vidondo mikononi mwake na ubavuni.

John 20:21

amani iwe nanyi

hii nisalamu ya kawaida

Kama vile Baba alivyonituma mimi, vivyo hivyo nami nawatuma ninyi...akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu"

Mungu Baba alimtuma Mungu Mwana anayewatuma waumini katika nguvu ya ya Mungu Roho.

Baba

Hiki ni cheo muhimu cha Mungu

watasamehewa

"Mungu atawasamehe"

Watafungiwa

"Mungu hatawasamehe"

John 20:24

Pacha

Tazama tafsiri tok Yohana 11:15

yule mwanafunzi mwingine walimwambia baadaye

neno "yule" linamaanisha Thomaso

Kma staona alama za misumari sitamini

Nitaamini tu pale nitakapoona alama za misumari na ubavu wake

Mikononi mwake

Neno "mwake" linamaanisha Yesu

John 20:26

Wanafunzi wake walikuwa chumbani tena

Neno "wake" linamaanisha Yesu

Amani na iwe nanyi

Hii ni salamu ya kawaida

asiyeamini

bila imani

John 20:28

umeamini

"umeamini kuwa niko hai"

pasipokuona

"ambao ambao hawajaniona nikiwa hai

John 20:30

ishara

Hii inamanisha miujiza inayotumika kuonyesha ushahidi kuwa Mungu ana nguvu zote na ambaye ana mamalaka kamili juu ya ulimwen

Mwana wa Mungu

Hiki ni cheo muhimu cha Mungu

Uzima katika jina lake

"Munaweza kuwa na uzima katika jina lake"

uzima

hii inamaanisha maisha ya kiroho

John 21

Yohana 21 Maelezo ya Jumla

Mifano muhima ya usemi katika sura hii

Mifano

Yesu anatumia mifano mingi ya uchungaji. Kwa mfano, "kulisha kondoo wangu," "chunga kondoo wangu" na "kulisha kondoo wangu." Petro sasa angekuwa mchungaji wa watu wa Mungu.

__<< | __

John 21:1

Baada ya mambo haya

"Baadaye kitambo"

na Tomaso aitwaye Didimasi

unaweza kutafsiri pia kwa kusema, "na Tomaso tuliyemwita Didimasi"

Didimasi

Maana ya jina hili ni "mapacha"

John 21:4

vijana

hii ni hali ya kusema rafiki zangu

mtapata wachache

maana yake, "mtakamata samaki wachache kwenye nyavu zenu"

tupeni ndani

vuteni nyavu ndani

John 21:7

aliyempenda

Huu ni upendo unaotoka kwa Mungu ambao hutazama zaidi mema ya wengine, hata kama hauna maslahi binafsi. Upendo wa aina hii huwajali zaidi wengine bila kujali wanachokifanya

(maana hakuwa amelivaa vizuri)

Hii ni kwa mujibu wa mukhutadha

Kwani hawakuwa mbali na pwani, yapata mita mia moja kutoka ufukweni)

Hii ni kwa mujibu wa mukhutadha

yapata dhiraa miambili

"mita tisini"dhiraa ni ndogo kuliko nusu mita

John 21:10

Simoni Petro kisha akaenda juu

Hii inamaanisha kuwa Petro alirudi kwenye mtumbwi

na akatoa nyavu nchi kavu

na akatoa nyavu na kuziweka ufukweni

nyavu ilikuwa haijararuka

Unaweza kutafsiri hii kama, "nyavu hazikuharibika

John 21:12

kifungua kinywa

mlo wa asubuhi

mara ya tatu

unaweza kutafsiri hii kama muda nambari tatu.

John 21:15

je, unanaipenda...wanipenda mimi

Hapa "upendo" linamanisha aina ya upendo unaotoka kwa Mungu, amabao unaangalia mema ya wengine, hata pale ambapo hakuna maslahi binafsi

wewe wajua kuwa mimi na kupenda wewe

Petro anajibu, anatumia neno kwa "upendo" ambalo linonyesha upendo kwa ndugu au upendo wa urafiki au upendo wa kifamila.

Lisha wanakondoo wangu

"Lisha watu wangu ninaowajali"

Chunga kondoo wangu

"Wajali watu wangu ninaowajali"

John 21:17

Je, wanipenda mimi?

Mara hii Yesu anapouliza swali hili anatumia neno kwa "upendo" ambalo linamanisha upendo wa ndugu au upendo wa urafiki au upendo wa kifamila

Lisha kondoo wangu

"Uwajali watu wangu ninaowajali"

Kweli, kweli

itafsiriwe kama ilivyo kwenye Yohana 1:49, 1:51

John 21:19

Sasa

Yohana analitumia neno hili kuonyesha kuwa anatoa maelezo ya mukhutadha kabla hajaendelea na simulizi

John 21:20

alimpenda

Huu ni aina ya upendo amabao hutoka kwa Mungu ambao huangalia mema ya wengine hata kama hauna maslahi binafsi. Aina ya upendo huu huwajali wengine, bila kujali wanachokifanya

kwenye chakula cha jioni

Hii inakumbushia chakula cha mwisho ambacho Yesu alikula na wanfunzi wake

Petro alimwona

Hapa neno "yeye" linalemlenga "mwanafunzi ambaye Yesu alimpenda"

John 21:22

nataka abaki

Hapa "yeye", "a...ki", linamanisha "mwanafuzi ambaye Yesu alimpenda" Tazama 21:20

Nitakapokuja

Inamaaninisha kur duniani kwa Yesu mara ya pili, atakapokuja kutoka mbinguni.

hilo linakuhusu nini?

"usijihusishe na jambo hilo"

ndugu

Yesu ana anatumia neno hili kwa wanafuzi wake kama nduguze.

John 21:24

Taarifa za jumla:

Huu ndio mwisho wa Injili ya Yohana. Hivyo mwandishi ambaye ni Yohona anatoa salamu za mwisho na kusema kidogo kuhusiana na yeye mwenyewe.

mwanafunzi

mwanafunzi wa Yohana

ambaye hushuhudia kuhusu mambo yaleyale

neno kushuhudia kama lilivyotumika hapa linamaanisha kuona kitu

sisi tunajua

"sisi" hapa inamaanisha wale wanaomwamini Yesu

kama kila kitu kingeandikwa

unaweza kutafsiri pia kwa kusema, "kama mtu angeandika kila kitu"

hata dunia pia isingeweza kutosha vitabu vyote

Yesu alifanya miujiza mingi kuliko ambavyo watu wangeweza kuandika kwenye vitabu

UTANGULIZI WA KITABU CHA MATENDO YA MITUME

Sehemu ya 1: Utangulizi wa Jumla

Muhtasari wa Kitabo cha Matendo ya Mitume

  1. Mwanzo wa kanisa na huduma yake(1:1-2:2:41)
  2. kanisa la kwanza Yerusalemu (2:42-6:7)
  3. kuongezeka kwa upinzani na mauaji ya kishujaa ya Stefano (6:8-7:60)
  4. Mateso ya Kanisa na utume wa Filipo (8:1-40)
  5. Paulo anakuwa Mtume (9:1-131)
  6. Utume wa Petro na Wakristo wa Kwanza Wayunani (9:32-12:24),
  7. Paulo, mtume wa Wayunani, Sheria ya Wayahudi na baraza la viongozi wa kanisa Yerusalemu.
  8. Ongezeko la kanisa katikati mwa inchi za karibu ya bahari Mediterane na Asia Ndogo (16:6-19:20)
  9. Paulo anasafiri Yerusalemu na kuwa mfungwa Roma (19:21-28:31)

Kitabu cha Matendo Ya Mitume kinazungumzia nini?

Kitabu cha Matendo Ya Mitume kinazungumzia habari ya Kanisa la Mwanzo kadiri ya lilivyoongezeka. Kinaashiria vile nguvu za Roho Mtakatifu zilivyosaidia kanisa la Kwanza. Matendo haya yanaanza pindi Yesu alipopaa mbinguni hadi miaka thelathini kutoka hapo.

Ni Jinsi gani jina la kitabo hiki kinafaa kutafsiriwa?

Watafsiri wanaweza kuchagua jina liliyotumiwa zamani kwa mfano, 'Matendo ya Roho Mtakatifu' Ama watafsiiri wanaweza kuchagua jina la waziwazi, kama 'Matendo ya Roho Mtakatifu kupitia kwa mitume'.

Nani aliandika kitabu cha Matendo ya Mitume?

Kitabu hakijamtaja mwandishi ingawa kinaelekezewa Tiofila, yule ambaye Mwinjili Luka anamzungumzia. Kitabu kinazungumzia "sisi" kuashiria kwamba mwandishi wake alisafiri na Paulo. Wasomi wengi wengi wa Biblia wanaamini kwamba ni Luka aliyekuwa akisafiri na Paulo. Ndio maana watu wengi wanaamini kwamba Luka ndiye mwandishi wa hiki kitabu na cha Injili Ya Luka.

Luka alikuwa daktari wa matibabu. Mfumo wake wa maandishi unamuashiria kama mtu aliyekuwa na masomo ya juu sana. Kuna uwezekano mkubwa hakuwa Myahudi. Aliyashuhudia matukio mengi yaliyotajwa katika kitabu cha Matendo.

SEHEMU YA 2:maswala muhimu ya kidini na kitamaduni

Kanisa ni nini

Kanisa na kundi la watu wanaomwamini kristu. Kanisa linajumlisha Wayahudi na wasiyo wayahudi (Wayunani). Matukio ya kitabu hiki kinaonyesha jinsi Mungu anavyolisaidia Kanisa ni. Aliwapa uwezo waumini kuishi kiadilifu kupitia kwa Roho wake Mtakatifu.

SEHEMU YA 3: Maswala muhimu ya Tafsiri

Ni mambo gani muhimu katika maandiko ya Matendo ya Mitume?

Yafuatayo ndio maswala muhimu katika Matendo ya Mitume:

Mistari ifuatayo inapatkana katika tafsiri za kitambo za Bibilia, lakini haiko katika nyaraka bora za kitambo za Bibilia. Tafsiri zingine za kisasa huweka mistari hii kwa mabano (). tafsiri za ULB na UDB huiweka kwa maelezo ya chini (footnote)

Katika maandiko yafuatayo,haijulikani yaliyosema maandiko ya awali, Watafsiri watahitajika kuchagua masomo yepi ya kutafsiri. ULB ina masomo ya kwanza lakini masomo yake ya pili yamewekwa kwenye maelezo ya chini.

(See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/jit.html#translate-textvariants

Acts 1

Matendo 01 Maelezo ya Jumla

Muundo na mpangilio

Sura hii inarekodi tukio,kawaida linajulikana kama "kupaa", wakati Yesu alirudi mbinguni baada ya ufufuko wake. Hatarudi tena mpaka "Ujio wake wa pili." (rejelea: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#heaven and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#resurrection).

Toleo la UDB limeweka maneno "Kwa mpendwa Theofila" kando na maneno mengine. Hii ni kwa sabau Waiingereza huanza kuandika barua namna hivi. Unaeza anza kitabu hiki jinzi watu huanza kuandika waraka katika mila yako.

Tafsiri zingine zinanukuu kutoka Agano la Kale kwenye kulia kwa ukurasa kuliko maandiko yote kwa jumla. ULB hufanya hivi kupitia nukuu mbili kutoka Zaburi 1:20

DHANA MAALUM KATIKA SURA HII

BATIZA

Neno "batiza" lina maana mbili katika sura huu. Inaashiria ubatizo wa Yohana na ubatizo wa Roho Mtakatifu (Matendo 1:5). (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#baptize)

"Alizungumza kuhusu ufalme wa Mungu"

Wasomi wengine huamini kuwa wakati Yesu "alipozungumzuia kuhusu ufalme wa Mungu," aliwaeleza wanafunzi wake ni kwa nini ufalme wa Mungu haukuja kabla ya kifo chake. Wengine huamini kwamba ufalme wa Mungu ulianza wakati Yesu alikuwa hai na ya kwamba hapa Yesu alikuwa anafafanua kwamba huu ulikuwa mwanzo kwa umbo jipya.

Matatizo mengine ya tafsiri katika sura hii.

wanafunzi kumi na wawili

yafuatayo ni majina ya wanafunzi kumi na wawili

Katika Injili ya Matayo

Wa kwanza Simoni aliyeitwa Petro, na Andrea nduguye; Yakobo wa Zebedayo, na Yohana nduguye; Filipo, na Bartholomayo; Tomaso, na Mathayo mtoza ushuru; Yakobo wa Alfayo, na Thadayo;Simoni Mkananayo, na Yuda Iskariote

Katika injili ya Marko

Simoni (Petro),Andrea,na Yakobo, mwana wa Zebedayo, na Yohana nduguye Yakobo, akawapa jina la Boanerge, maana yake, wana wa ngurumo; na Filipo, na Bartholomayo, na Mathayo, na Tomaso, na Yakobo wa Alfayo, na Thadayo, na Simoni Mkananayo, na Yuda Iskariote.

Katika injili ya Luka

Simoni(Petero),Andrea,Yakobo,Yohana,Filipo,Bartholomayo,Matayo,Tomaso,Yakobo wa Alfayo,Simoni Mkananayo,Yuda wa Yakobo na Yuda Iskariote.

Kuna uwezekano ya kwamba Thadayo na Yuda wa Yakobo ni mtu mmoja

Akeldama

Hili ni neno la Kihebrania au Kiaramaiki. Luka alitumia maneno ya Kigiriki ili wasomaji wake wajue lilivyotamkua,kisha akawaeleza maana yake. Unatakikana kulitamka jinsi linalatamkwa kwa lugha yako kisha ukaeleza maana yake.(Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-transliterate)

| >>

Acts 1:1

Sentensi unganishi.

Luka anaelezea ni kwasababu gani anamwandikia Theofilo

Kitabu cha zamani nilikiandika

Kitabu cha zamani ni Injili ya Luka.

Theofilo

Luka aliandika kitabu hiki kwa mtu anayeitwa Theofilo. Baadhi ya watafsiri hufuata mfumo wa tamaduni zao za kuelezea barua na huandika "Mpendwa Theofilo" mwanzoni mwa sentensi. Theofilo humaanisha "rafiki wa Mungu.

Mpaka siku alipopokelewa juu

Hii inarejesha kwenye kupaa kwa Yesu mbinguni

Amri kupitia kwa Roho Mtakatifu

Roho Mtakatifu alimwongoza Yesu kuwaelekeza mitume wake juu ya vitu fulani.

Baada ya kuteswa kwake

Hii inahusu mateso ya Yesu na kifo chake msalabani.

Alijidhihirisha Yeye mwenyewe akiwa hai

Yesu alionekana kwa mitume wake na kwa wanafunzi wengi wengine.

Acts 1:4

Sentensi unganishi

Tukio hili lilitukia wakati wa siku arobaini ambazo Yesu alionekana kwao baada ya Yeye kufufuka toka katika wafu.

Alipokuwa akikutana pamoja nao

Wakati Yesu alipokutana pamoja na mitume wake.

Ahadi ya Baba

Roho Mtakatifu ambaye Baba aliahidi kumtuma.

ambayo, alisema

Roho Mtakatifu ambaye Yesu alisema habari zake.

Yohana alibatiza kabisa kwa maji,

Yesu anatofautisha ubatizo wa Yohana wa maji, na ule ubatizo wa Mungu ambao utakuwa ni wa Roho Mtakatifu.

Yohana alibatiza kwa maji kabisa

"Yohana hasa alibatiza watu kwa maji"

ninyi mtabatizwa

"Mungu atawabatiza ninyi"

Acts 1:6

huu ni wakati wa utakaorudisha ufalme kwa Israeli

"Sasa Utafanya Israeli taifa lenye nguvu tena?"

nyakati au majira

"nyakati au tarehe"

mtapokea nguvu... na mtakuwa mashahidi wangu

Mitume watapokea nguvuitakayowasaidia kumshuhudia Yesu. "Mungu atawatia nguvi... kuwa mashahidi wake.

hadi miisho ya nchi

"kote duniani" au" mpaka sehemu za mbali sana za dunia"

Acts 1:9

wakiwa wanatazama juu

"mitume wakiwa wanaangalia juu mawinguni" wakati Yesu akiinuliwa na mawingu kwenda juu.

Yeye aliinuliwa juu

Mungu alimwinua juu ya anga

wingu likamficha toka katika macho yao

" na wingu liliwazuia kumwona hivyo wasingelimwona tena"

kuangalia kwa makini mbinguni

"Kutazama mawinguni" au "kukaza macho kwenye mawingu"

Ninyi wanaume wa Galilaya

Malaika anazungumza na mitume kama watu waliotoka Galilaya.

atarudi kwa namna ile ile

Yesu atarudi katika mawingu , kama ilivyokuwa wakati wa kupaa kwake kwenda mbinguni.

Acts 1:12

Ndipo wao wakarudi

"Mitume wakarudi"

mwendo wa siku ya sabato

Hii inaelezea umbali ambao kutokana na desturi za walimu wa sheria wa kiyahudi, mtu aliruhusiwa kutembea mwendo wa sabato ambao yapata kilomita moja hivi.

Walipowasiri

"Walipofika mwisho wa safari yao. Mstari wa 12 unasema, "Ndipo wakarudi Yerusalemu kutoka kwenye mlima wa mizeituni"

chumba cha juu

"chumba ambacho kipo juu kwenye nyumba"

Walikuwa wameungana kama mtu mmoja

Kikundi kiliungana na hakikuwa na mgawanyiko au migongano.

wakiwa na juhudi wakiendelea katika kuomba

Wanafunzi waliomba kwa pamoja kwa kawaida na mara kwa mara.

Acts 1:15

Sentensi unganishi

Tukio hili lilitukia wakati Petro na waumini wengine walikuwa pamoja katika chumba cha juu.

Katika siku zile

Maneno haya yanaashiria mwanzo mpya wa historia. Yanaelezea kipindi baada ya Yesu kupaa na wakati wanafunzi wakiwa katika chumba cha juu wamekutanika kuomba.

katikati ya ndugu

Neno "ndugu" Linaelezea ndugu waumini likiunganisha wanawake kwa wanaume.

ilikuwa lazima kwamba maandiko yatimizwe

Yale mambo tunayoyasoma katika maandiko lazima yatimizwe

kwa kinywa cha Daudi

Neno "kinywa" Linaelezea yale maneno aliyoyasema Daudi.

Acts 1:17

Sentensi unganishi

Katika mstari 17 Petro anaendelea na hotuba yake kwa waumini.

Maelezo ya Jumla:

Ingawa Petro anaongea na kundi lote la waumini waliokuwa chumba cha juu, lakini neno "sisi" analitumia kwa kuwataja mitume pekee waliotembea, kuketi, kuongea na Yesu tangu mwanzo wa huduma yake hadi kupaa kwake mbinguni.

Sasa mtu huyu

Neno "mtu huyu" linaelezea juu ya Yuda Iskariote.

alichokipokea kwa uovu wake

"pesa alizopokea ni malipo ya ya uovu alioufanya"

hapo alianguka akitanguliza kichwa, mwili ukapasuka na matumbo yake yote yakawa wazi yakamwagika.

Kuanguka kwa Yuda kulisababisha mwili wake kupasuka na matumbo kumwagika.

shamba la damu.

Watu waliokuwa wakiishi Yerusalemu waliposikia habari za Yuda na kifo chake, wakaliita jina lile shamba lililonunuliwa kwa fedha hizo kuwa ni shamba la damu.

Acts 1:20

Sentensi unganishi:

Petro anaendeleza hotuba yake kwa waumini ambayo alikuwa ameianza.

Maelezo ya Jumla:

Ujumbe wake unasimulia vile Yuda alivyotenda akiunganisha na unabii wa maandiko, Petro anarejea ujumbe katika kitabu cha Zaburi kwamba anaamini inahusiana na tukio hilo.

Kwa sababu imeandikwa katika Kitabu cha Zaburi

Petro anathibitisha kuwa, "Daudi aliandika katika kitabu cha Zaburi".

'Ngoja eneo lake liwe hame na isiruhusiwe hata mmoja kuishi pale

Ni hali ya eneo kuachwa ukiwa kutokana na chanzo cha historia yake.

na isiruhusiwe hata mtu mmoja kuishi pale

Kiwanja ni najisi (mwiko/haramu) au haifai kuishi juu yake.

Ngoja mtu mwingine achukue nafasi yake ya uongozi

"Anaweza akarithiwa katika nafasi ya uongozi"

Acts 1:21

Sentensi Unganishi:

Petro anamaliza hotuba yake kwa waumini aliyoianza

Maelezo ya jumla

Neno "sisi" Petro analitumia akimaanisha mitume na siyo waumini wote.

lazima awe shahidi wa ufufuo pamoja nasi

Petro anawaambia mtu atakayechukua nafasi awe na sifa hizo.

watu walioabatana nasi ... mmoja wao hao lazima awe shahidi pamoja nasi wa kufufuka kwake

Petro anafafanua sifa kwaajili ya mtu ambaye atamrithi Yuda kama mtume.

Wakaweka mbele watu wawili

Walipendekeza majina ya watu wawili waliokuwa na sifa sawa na hotuba ya Petro.

Yusufu aliyeitwa Barsaba, ambaye pia aliitwa Yusto

Yusufu pia alijulikana kwa majina Barsaba na Yusto alitwaa nafasi iliyokuwa imeachwa wazi na Yuda Iskariote.

Acts 1:24

Waliomba wakisema

"Ndipo waumini waliomba" Inamaanisha wote waliokuwemo chumba cha juu waliomba, pengine kwa kuongozwa na mtume mmoja.

Wewe, Bwana, wajua mioyo ya watu wote

"Bwana, Wewe wajua msukumo wa ndani na mawazo ya kila mmoja"

hivyo funua yupi kati ya hawa wawili ndiye uliye mteua kuchukua nafasi katika huduma hii ya kitume

"Kwa sababu hiyo, Mungu, tuoneshe sisi yupi kwenye watu hawa wawili umemteua kujaza nafasi hii wazi katika matume"

Kutokana na Yuda kukosea na kwenda njia yake mwenyewe

Nafasi iliachwa wazi sababu Yuda alimsaliti Yesu, aliondoka, na akafa.

Wakawapigia kura

Walitumia kura kuamua kati ya Yusufu na Mathiasi

Kura ikamwangukia Mathiasi

Kura iliashiria kwamba Mathiasi alikuwa amechaguliwa kuchukua nafasi ya Yuda

Alihesabiwa pamoja na mtume kumi na mmoja

"wanafunzi walimchukulia kuwa ni mmoja wa mitume"

Acts 2

Matendo 02: Maelezo ya Jumla

Muundo na mpangilio

Tafsiri zingine zimesongeza kila mstari wa ushairi mbali kulia kuliko maandiko mengine ili isomeke kwa urahisi. ULB hufanya hivi kutumia ushairi ulionukuliwa kutoka Agano La Kale katika 2:17-21,25-28 na 34-35.

Tafsiri zingine zimenukuu kutoka Agano la Kale katika mkono wa kulia wa ukurasa mbali na maandishi mengine. ULB hufanya hivi kutumia nukuu ya 2:31

Matukio yanayofafanuliwa katika sura hii huitwa "Pentekoste." Watu wengi huamini kwamba kanisa lilianza wakati Roho Mtakatifu alikuja kuishi ndani ya waumini katika sura hii.

HANA MAALUM KATIKA SURA HII

NDIMI

Neno "ndimi" lina maana mbili katika sura hii. Luka anaelezea kilichoshuka kutoka mbinguni (Matendo 2:3) kama kilichofanana na ndimi za moto. Hii ni tofauti na "ulimi wa mwale," ambao ni moto unaofanana na ulimi. Luka pia anatumia neno "ndimi" kuelezea lugha walizozungumza watu baadaya kujazwa na Roho Mtakatifu (Matendo 2:4-6).

SIKU ZA MWISHO

Hakuna ajuaye wakati "Siku za mwisho" (Matendo 2:17) zilipoanza. Tafsiri yako lazima isielezee zaidi ya ULB inavyoeleza. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lastday)

Batiza

Neno "batiza" katika sura hii linaashiria ubatizo wa Wakristo (Matendo 2:38-41). Ingawa tukio lililotajwa katika Matendo 2:1-11 ni ubatizo wa Roho Mtakatiu ambao Yesu aliahidi katika Matendo (1:5, neno "batiza" hapa halikuashiria hilo tukio (tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#baptize).

Unabii wa Yoeli

Utabiri mwingi wa Yoeli ulitimilika katika siku ya Pentekoste (Matendo 2:17-18), lakini vitu vingine alivyosema Yoeli havikutendeka (Matendo 2:19-20). (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#prophet)

Maajabu na ishara

Haya maneno yanaashiria mambo ambayo Mungu pekee yake angeyatenda kuonyesha kwamba Yesu ndiye yule wanafunzi wake walinena juu yake.

<< | >>

Acts 2:1

Maelezo ya Jumla

Hili ni tukio jipya; hii sasa ni siku ya Pentekoste, siku 50 baada ya pasaka.

Maelezo ya jumla

Neno "wao" huenda linarejea kwenye kundi la mitume na waumini wengine 120 ambao walikuwa pamoja katika. Luka 1:15 ametaja vile.

Ghafla

Neno hili linatumika hapa kuonesha tukio lililotokea pasipo kutegemea.

hapo ikaja sauti kutokea mbinguni

"kelele ilitokea mawinguni mahali pa makao ya Mungu"

Sauti kama uvumi wa nguvu wa upepo

"kama uvumi wa upepo wa nguvu sana" au kama mvumo wa nguvu"

Nyumba yote

Hii inaweza ikawa nyumba au jengo kubwa.

Kulionekana kwao ndimi kamaza moto

Hizi si ndimi hasa au moto 1) ndimi zilizoonekana kama za moto au 2) mwale mdogo wa moto ulioonekana kama ndimi wakati unawaka katika sehemu ndogo, kama vile chemli , mwale unaweza ukajitengeneza kama ulimi.

Wote walijazwa na Roho Mtakatifu

Hii inaweza kutafsiriwa kama kitenzi tendaji. Roho Mtakatifu aliwajaze wote waliokuwa kwenye hicho chumba.

Acts 2:5

Maelezo ya jumla

Mstari wa 5 unatoa taarifa ya nyuma kuhusu idadi kubwa ya wayahudi ambao walikuwa wanaishi Yerusalemu, wengi wao walikuwapo wakati wa tukio hili.

Maelezo ya jumla

Hapa neno "wao" linajumuisha waumini na neno "yake" linataja kila mtu katika kundi.

watu wa Mungu

watu waliotaka kuheshimu na au kumwabudu Mungu

kila taifa chini ya mbingu

"kila taifa duniani" Watu kutoka mataifa mbalimbali walikuwa wamekuja Yerusalemu.

Wakati sauti hii iliposikika

Hii inarejea sauti ambayo ilikuwa kama upepo wa nguvu kuwa: "Waliposikia sauti hii"

Mkusanyiko

"kundi kubwa la watu"

Walishangaa kwa mshangao mkuu

Maneno haya yana maana moha. Mshangao wao ulikuwa mkuu sana.

Kweli, hawa wote wanaoongea siyo Wagalilaya?

Watu waliuliza swali wakionyesha mshangao wao kuwa hawa ni wa eneo moja na lugha yao ni moja iweje waongee na lugha za mataifa yetu?

Acts 2:8

Kwa nini sisi tunawasikia, kila mmoja katika lugha tulizozaliwa nazo?

Inawezekana ikamaanisha 1) ni swali halisi ambalo watu walihitaji jibu lake kutokana na mshangao wao au 2) swali lisilohitaji jibu lililodhihirisha jinsi walivyoshangaa.

Waparthi ... Waelamu

Hii inaorodhesha baadhi ya mataifa, mikoa na miji ambayo watu walitoka.

Wabadili dini kufuata desturi za kiyahudi

"watu wasio Wayahudi ambao wamekuwa Wayahudi" au "waliogeukia dini ya Kiyahudi"

Acts 2:12

wameduwaa na kutatanishwa;

Watu hawakujua nini cha kufikiri kuhusu kilichokuwa kinatokea. "shangazwa na kuchanganyikiwa."

Hawa wamejazwa kwa mvinyo mpya."

Baadhi ya watu waliwatuhumu waumini kwa kile kilichotokea wakidai wamelewa na mvinyo.

mvinyo mpya

Linaelezea mvinyo unaoandaliwa kuwa na nguvu kuliko mvinyo ya kawaida

Acts 2:14

Sentensi unganishi:

Petro anaanza kuwasilisha hotuba yake kwa Wayahudi siku ya Pentekoste.

alisimama pamoja na wale kumi na mmoja

Mitume wote walisimama kuunga mkono hoja ya Petro

hili lijulikane kwenu, sikilizeni kwa makini

Petro anaelezea tukio ambalo watu wamelishuhudia likiendelea. Wamsikilize kwa makini

saa hizi ni asubuhi saa tatu.

"saa tatu za asubuhi. Petro anawafikirisha wasikilizaji wajue kuwa watu hawanyi wala hawalewi muda huo wa mapema katika siku.

Acts 2:16

Maelezo ya jumla

Petro anaendelea na hotuba yake kwa Wayahudi akiwakumbusha unabii wa nabii Yoeli katika Agano la Kale kwamba tukio hilo linalingana na utabiri huo.

Hiki ndicho kilichosemwa kupitia nabii Joeli

"hiki ni kile ambacho Mungu alisema na alimwabia Nabii Yoeli aandike mambo ambayo Mungu alikwishasema"

kumimina Roho wangu juu ya miili yote

Hii ni tamathali ya usemi ikizungumzia jinsi Mungu siku za mwisho atamtoa Roho Mtakatifu kwa wingi kwa watu wote.

Acts 2:18

Sentensi unganishi

Petro anaendelea kumnukuu nabii Joeli.

watumishi wangu na watumishi wangu wa kike

Wote waume kwa wake ni watumishi. Mungu atamwaga Roho wake kwa watumishi wake wote kwa wanaume na kwa wake.

Nitammimina Roho wangu

Mungu anamtoa Roho wake kwa ukarimu kwa watu wote.

toa unabii

Mungu anawatia msukumo kuizungumza kweli ya Mungu.

mafusho ya moshi.

"umande" au "ukungu"

Acts 2:20

Sentensi unganishi

Petro anahitimisha kumnukuu nabii Joeli.

Jua litageuzwa kuwa giza

Inamaanisha kwamba, jua litaonekana kuwa jeusi badala ya kutoa nuru.

na mwezi kuwa damu

Inamaanisha kwamba, mwezi utaonekana mwekundu kama damu.

Ya ajabu

"Si ya kawaida" au "muhimu"

kila mmoja ambaye huliitia jina la Bwana ataokoka

"Bwana atamwokoa kila mmoja ambaye anamwita"

Acts 2:22

Sentensi unganisha

Petro anaendelea na hoja yake kwa Wayahudi aliyoianza

sikieni maneno haya

"Sikilizeni kwa yale ninayotaka kuwaambia"

aliyethibitishwa na Mungu kwenu kwa matendo ya uweza na maajabu, na ishara

Inamaanisha Mungu anathibitisha kuwa alimchagua Yesu kwa huduma yake ya kudhihirisha matendo makuu ya miujiza.

mwanadamu aliyethibitishwa na Mungu kwenu

"Mtu ambaye Mungu alimdhibitisha kwenu"

Kwa sababu ya mpango uliokusudiwa tangu mwanzo, na maarifa ya Mungu

Inamaanisha kuwa, Mungu alipanga na kujua tangu zamani kwamba yangetokea nyakati za Yesu

ambaye Mungu alimwinua

Maana yaweza kuwa: 1) "Mlimtia Yesu katika mikono ya maadui" au 2) Yuda alimsaliti Yesu kwenu"

kwa mikono ya watu wahalifu, mlimsulibisha na kumuua

Ingawa watu wahalifu kweli walimsulibisha Yesu, hapa Petro anawashitaki kundi lote kwa kumwua kwasababu walikuwa wamekusudia Yesu auawe.

akauondoa uchungu wa mauti kwake, kwasababu haikuwezekana kwake kumilikiwa na huo.

etro anazungumzia kifo kama mfano wa binadamu anayeshikilia wafungwa hara kusababisha mateso makali.

Acts 2:25

Maelezo ya jumla

Petro ananukuu kifungu ambacho Daudi alikiandika katika Zaburi kinachotaja kuteswa kwa Yesu na kufufuka kwake.

Maelezo ya jumla

Tangu Petro ataje kwamba Daudi alitangulia kusema maneno kuhusu Yesu, maneno "Mimi na Yangu" yanamtambulisha Yesu. Na maneno Bwana na Yeye" yanamtambulisha Mungu.

mbele ya uso wangu

Linamaanisha, "Mbele yangu au mbele ya uwepo wangu"

pembeni mkono wangu wa kulia

Mkono wa kulia ulifikiriwa kuwa ni wa nguvu sana. Mtu aliye mkono wa kuume alikuwa ama mtumishi mwenye nguvu sana au msaidizi mwenye uwezo sana.

moyo wangu ulikuwa na furaha na ulimi wangu ulishangilia.

NI: "Nilikwa na furaha na kushangilia"

mwili wangu utaishi katika ujasiri

"Ingawa hata mimi ni wa kufa tu, nitakuwa na ujasiri kwa Mungu"

Acts 2:27

Sentensi unganishi

Petro anamaliza nukuu ya Daudi.

Maelezo ya jumla

Petro anasema, Daudi alisema maneno kuwa Mtakatifu wangu akimaanisha Yesu na maneno "wako" akimaanisha Mungu.

wala hutaruhusu Mtakatifu wako kuona uozo

Mwili wake Masihi hautabaki maiti muda mrefu mpaka uoze. au "kuchakaa"

njia za maisha

"kweli yenye-kuhuisha"

nijae furaha mbele ya uso wako.'

Neno "Uso" anamaanisha uwepo wa Mungu.

furaha

"Shangwe au Kicheko"

Acts 2:29

Sentensi unganishi

Petro anaendelea na hotuba yake aliyoianzisha kwa Wayahudi wanaomzunguka na kwa waumini wengine wa Yerusalemu.

yeye alikufa na akazikwa

"He died and people buried him"

kwamba ataweka mmoja katika uzao wake kwenye kiti cha enzi

"Mungu angemtuma mmoja wa uzao wa Daudi juu ya kiti cha enzi cha Daudi"

Aliliona hili mapema

Mungu alijua hata kabla lilikuwa halijatokea.

wala alikuwa hakuachwa kuzimu

Mungu hakumwacha Yesu kuzimu.

wala mwili wake haukuoza.'

Mwili kuoza kunamaanisha kuteketea baada ya kifo. hivyo Mungu hakumwacha Yesu muda ambao hatA mwili wake uteketee.

Acts 2:32

Maelezo ya Jumla

Neni "sisi" linaelezea wanafunzi na wale wotewaliokuwa mashahidi wa kufufuka kwa Yesu baada ya kifo chake.

Mungu alimfufua

Neno "alimfufua" Linaelezea kuwa Mungu alimfufua Yesu kutoka kwa wafu.

akiwa ameinuliwa katika mkono wa kuume wa Mungu

Mungu alimwinia Yesu juu katika mkono wake wa kuume.

yeye amemimina hii ahadi,

Neno "mimina" lina maana Yesu ambaye ni Mungu amefanya tukio hili litokee la kumtoa Roho Mtakatifu kwa waumini.

Acts 2:34

Sentensi unganishi

Petro anamaliza hotuba yake kwa Wayahudi aliyoianza

Maelezo ya jumla

Petro tena ananukuu moja ya Zaburi za Daudi. Daudi hazungumzi kwa nafsi yake mwenyewe katika zaburi hii bali anazungumzia juu ya Yasu Masihi.

mpaka nitakapowafanya adui zako kigoda kwa ajili ya miguu yako

Inamaanisha Mungu atafanya ushindi mkamilifu wa maadui wa Masihi na kuwaweka chini yake.

nyumba yote ya Israeli

Inamaanisha taifa zima la Israeli.

Acts 2:37

Sentensi unganishi

Wayahudi wanaitikia hotuba ya Petro na Petro anawajibu.

waliposikia hivyo

"wakati watu waliposikia Petro akisema"

wakachomwa katika mioyo yao

"Maneno ya Petro yaliwachoma mioyo yao" au "kusikia hatia moyoni na kujawa na huzuni"

kubatizwa

"Turuhusu tupate kubatizwa"

Ni ahadi kwaajili yako

"Ahadi ni kwaajili yako"

wale wote walioko mbali

"WAtu wote waliombali na Mungu mioyoni mwao.

Acts 2:40

Sentensi unganishi

Huu ni mwisho wa sehemu ya habari kwa tukio la siku ya Pentekoste. Inaanza sehemu nyingine inayoelezea jinsi gani waumini waliendelea kuishi baada ya siku ya Pentekoste.

alishuhudia na kuwasihi

"Aliwaambia waziwazi na kuwasihi waitikie kwa ujumbe alioutoa kwao.

Jiokoeni mtoke katika kizazi hiki kiovu

Wajiokoe kutoka katika adhabu ya Mungu itakayowapata watu waovu.

wakayapokea maneno yake

Inamaanisha wakayapokea maneno aliyoyasema Petro kuwa yalikuwa ya kweli.

Walibatizwa

Wote walioamini walibatizwa.

hapo wakaongezeka katika siku hiyo kama watu elfu tatu

"watu wapatao elfu tatu waliongezeka"

katika kuumega mkate

Walishiriki na kula chakula kwa pamoja

Acts 2:43

Hofu ikaja juu ya kila nafsi

watu walijawa na hofu na kicho cha Mungu ndani yao

maajabu mengi na ishara zikafanyika kupitia mitume

Mungu alifanya miujiza na ishara nyingi kupitia wanafunzi wake.

wote walikuwa pamoja

Inaweza kuwa, "wote waliamini jambo hilo moja" au " waumini wote walioamini walikuwa pamona katika sehemu moja"

walikuwa na vitu vyote kwa ushirikiano

"walitumia mali zao kwa kumgawia kila mmoja na mwenzake"

mali walizo miliki

Mashamba na vitu vingine vilivyokuwa wanavimiliki.

kugawanya kwa wote kulingana na hitaji la kila mmoja.

Kila mmoja aligawiwa kulingana na uhitaji wake.

Acts 2:46

waliendelea wakiwa na lengo moja

Waumini waliendelea kukutana pamoja, kwa kusudi moja.

walimega mkate kwenye nyumba zao

walishirikiana kula chakula chao katika nyumba zao na pia kula chakula cha Bwana kwa pamoja.

kwa furaha na unyenyekevu wa moyo

Hii inamaana bila kiburi, kwa furaha, bila choyo na bila kuangalia cheo au upendeleo.

wakiwa na kibali na watu wote

"Watu wote waliwakubali"

ambao walikuwa wakiokolewa

Ambao Bwana alikuwa akiwaokoa

Acts 3

Matendo 03 Maelezo kwa jumla

Dhana maalum katika sura hii

Agano Mungu aliagana na Abrahamu

Sura hii inaeleza kwamba Yesu alikuja kwa Wayahudi kwa sababu Mungu alikuwa akitimiza sehemu yake ya agano lake na Abrahamu. Petero alifikiri kwamba Wayahudi ndio waliokuwa na hatia ya kumuua Yesu.

Tafsiri zingine za utata katika sura hii

"Mliyemtia mikononi mwa wakuu"

Warumi ndio waliomuua Yesu, lakini walimuua kwa sababu Wayahudi walimkamata, wakamleta kwa Warumi, wakawaambia wamuue. Kwa sababu hii, Petero alifikiri kwamba hao ndio waliokuwa na hatia ya kumuua Yesu. Lakini anawaeleza yakwamba hao ndio wa kwanza ambao Mwenyezi Mungu ametuma wafuasi wa Yesu kuwakaribisha watubu (Luka 3:26). (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#repent)

<< | >>

Acts 3:1

Sentensi unganishi

Siku moja; Petro na Yohana wanakwenda hekaluni

Maelezo ya jumla

Mstari wa 2 unatoa mazingira juu ya mtu aliyekuwa kiwete.

ndani ya hekalu

"katika eneo la hekalu" au "katika hekalu." walikuwa hawakuenda ndani ya jengo la hekalu ambamo makuhani waliotumika tu ndio walikuwa wanaruhusiwa.

Mtu fulani, kiwete tangu kuzaliwa, alikuwa akibebwa kila siku na alikuwa akilazwa katika mlango wa hekalu.

Kila siku watu walikuwa wakimbeba mtu huyo na kumlaza karibu na mlango wa hekalu.

Kiwete

Asiyeweza kutembea

mlango wa hekalu ulioitwa mzuri

Mlango wa hekalu uliokuwa ukiitwa mzuri.

Acts 3:4

Petro, akimkazia macho

"Petro na Yohana walimwangalia mtu huyo kwa makini na Petro akaongea"

Kiwete akawaangalia

"kiwete aliwatazama Petro na Yohana kwa makini"

Fedha au dhahabu

Fedha au dhahabu ilitimika kuwakilisha pesa.

kile nilichonacho

Inafahamika kuwa Petro alikuwa na uwezo wa kumponya yule mtu.

katika jina la Yesu Kristo

"Kupitia mamlaka na nguvu ya Jina la Yesu Kristo" lilimponya mtu yule.

Acts 3:7

aliingia ... katika hekalu

Hakuingia ndani ya hekalu mahali makuhani pekee wanaruhusiwa kuingia. Yeye aliingia kwenye uwanda wa hekalu

Acts 3:9

Wakatambua kwamba alikuwa ni yule mtu

Kila mmoja alishuhudia kuwa aliyeponywa ndiye alikuwa mtu yule.

Lango la uzuri

Hili lilikuwa moja ya jina la milango ya kuingia kwenye eneo la hekalu.

walijawa na mshangao na kustaajabu

Watu walishikwa na mshangao mkubwa.

Acts 3:11

Sentensi unganishi

Baada ya kuponywa kwa mtu aliyekuwa hawezi kutembea, Petro anaongea na umati.

Maelezo ya jumla

Katika ukumbi uluokuwa ukiitwa Solomoni. Hapa iko wazi kuwa Petro alitumia eneo hili kutoa hotuba yake, haikuwa ndani ya hekalu ambamo ni makuhani tu walioruhusiwa kuingia.

maajabu makuu

"kujawa na mshangao" au "Kaduwaa"

Wakati Petro alipoona hiki

"Petro alipoona mkutano unaongezeka na kuzidi kushangaa.

Ninyi watu wa Israeli

"Waisraeli wenzangu". Petro akizungumza na mkutano. Neno "watu" katika mkutadha huu inahusisha kila mmoja aliyepo.

kwa nini mnashangaa?

Petro anauliza swali hili ili kuwaambia watu wasishanganzwe na kile kimetokea.

Kwa nini mnayaelekeza macho yenu kwetu, kama kwamba tumemfanya huyu atembee kwa nguvu zetu wenyewe au uchaji wetu?

Petro anawauliza swali hili ili kuwathibitishia kuwa tukio hilo halikutendwa na wao yaani Petro na Yohana, hivyov wasiwatazame wao kama ndiyo waliomponya yule kiwete.

Acts 3:13

Sentensi unganishi

Petro anaendelea na hotuba yake kwa Wayahudi aliyoianza

ambaye mlimkabidhi

"ambaye mlimkamata na kumkabidhi kwa Pilato"

na kumkataa mbele ya uso wa Pilato

"yeye mlimkataa mbele ya Pilato "

yeye alipoamua kumweka huru

"Pilato alipoamua kumweka Yesu huru"

badala yake mkataka muuaji aachwe huru.

"Mlimtaka Pilato amfungulie muuaji"

Acts 3:15

Maelezo ya jumla

Neno "sisi" linawajumuisha Petro na Yohana.

Mfalme wa uzima

Neno hili linamtaja Yesu "Ni mmoja awapaye watu uzima wa milele au "Mtawala wa maisha"

Sasa

Neno hili lilitumika kuhamisha usikivu wa mkutano kwa yule kiwete

kwa imani katika jina lake

Kiwakilishi "Jina" ni jina la Yesu.

amempatia mtu huyu nguvu

"amemfanya mtu huyu nguvu ya kupona"

Acts 3:17

Sasa

Hapa Petro anageuza usikivu wa mkutano kutoka kwa kiwete na anaendelea kuwaambia moja kwa moja.

kwamba mlitenda katika ujinga

Maana inayowezekana 1) Hao watu hawakujua kuwa Yesu alikuwa Masihi au 2) Watu hawakujua maana ya kile walichokuwa wakifanya.

Mungu aliwaambia mapema kwa vinywa vya manabii wote

Manabii waliponena, ilikuwa kama Mungu mwenyewe aliyenena kwasababu aliwaambia nini cha kusema.

kwa mdomo wa manabii wote

Inamaanisha yale yote yaliyonenwa "kupitia manabii" na kuyaandika.

Acts 3:19

Tubuni ... na kugeuka

"Kutubu na kugeuka kunamaanisha kubadirisha njia ya mtazamo na fikra zao kutoka katika dhambi na wamgeukie Mungu"

ili kwamba dhambi zenu ziweze kuondolewa kabisa

"kufuta" au "iliyoondolewa" ili Mungu aweze kuzifuta dhambi zao.

kusudi zije nyakati za kuburudika kutokana na uwepo wa Bwana

"Muda wa kuburudishwa katika uwepo wa Bwana inaweza kuwa; 1) Muda ambao Mungu anaziimarisha roho za watu wake; 2) Muda ambao Mungu analeta uamsho kwenu.

kwamba aweze kumtuma Kristo

"Kwamba anaweza tena kumtuma Kristo". Huu ni ujio mwingine wa Yesu Kristo.

ambaye ameshateuliwa kwa ajili yenu

Mungu alishamteua Yesu kwa ajili yao.

Acts 3:21

Sentensi ungaishi:

Petro anaendelea na hotuba yake kwa Wayahudi waliokuwa wamesimama kwenye eneo la hekalu.

Maelezo ya Jumla

Katika mistari ya 22-23 Petro ananukuu mambo fulani Musa alisema mapema kuhusu Masihi.

mbingu lazima zipokee

Ni mmoja ambaye mbingu lazima zimpokee. Petro anazungumza na mbingu kama anaongea na mtu aliyempokea Yesu nyumbani mwake.

mpaka wakati wa kurejeshwa kwa vitu vyote

"hadi wakati ambao Mungu atarejesha vitu vyote"

ambavyo Mungu alizungumzia zamani za kale kwa vinywa vya manabii watakatifu

"Mungu aliwaambia watakatifu wake manabii kuzungumzia habari zao"

manabii watakatifu ambao wamekuwapo tangu zamani za kale

"manabii wake watakatifu ambao waliishi zamani sana"

atainua nabii

"atateua mmoja kuwa nabii"

Itatokea kwamba kila mtu ambaye hasikilizi kwa nabii huyo ataangamizwa kabisa

mtu asiyemsikiliza Nabii ambaye Mungu amemtuma atamwangamiza kabisa.

Acts 3:24

Sentensi unganishi

Petro anahitimisha hotuba yake kwa Wayahudi aliyoianza

Ndiyo, na manabii wote

"Ni dhahili manabii wote" Neno hapa "ndiyo" linaongeza msisitizo kwa kile kinachofuata.

tokea Samweli na wale waliofuata baada yake

"wale manabii ambao walifuata baada ya uhai wa samweli"

siku hizi

"siku hizi" au "mambo ambayo yanatokea sasa"

Ninyi ni wana wa manabii na wa agano

"ninyi ni warithi wa manabii" na "ninyi ni warithi wa agano."

katika mbegu yako

"kwasababu ya uzao wako"

familia zote za dunia zitabarikiwa.'

Anamaanisha mataifa mbalimbali yatabarikiwa kwa ajili yake.

Baada ya Mungu kumwinua mtumishi wake,

"Baada ya Mungu kumchagua mtumishi wake" au "Baada ya Mungu kutoa mamlaka kwa mtumishi wake"

mtumishi wake

Hii inarejea kwa Masihi wa Mungu, Yesu.

Acts 4

Matendo 04 Maelezo kwa jumla

Muundo na Mpangilio

Tafsiri zingine zimetenga kila mstari wa ushairi kulia zaidi kuliko maandishi mengine ili isomeke vyema.ULB hufanya hivi na ushairi ulionukuliwa kutoka Agano la kale 4:25-26

DHANA MAALUM KATIKA SURA HII

umoja

Wakristo wa kwanza walitamani sana kuwa na umoja, Walitaka kuamini mambo sawa na kusaidiana kwa kila kitu walichokimiliki huku wakisaidia pia waliohitaji.

"Ishara na Maajabu"

Maneno haya yanaashiria vitu ambavyo vinaeza kufanywa tu na Mungu. Wakristo walitaka Mungu afanye yale tu ambayo angeweza kuyafanya ili watu waamini kwamba waliyoyanena kumhusu Yesu yalikuwa ya ukweli.

Mifano muhimu kwenye hii sura

Jiwe la pembeni

Jiwe la pembeni lilikuwa kipande cha jiwe kilichowekwa chini wakati wa ujenzi wa jengo. Neno hili limetumika kumaanisha sehemu muhimu ya kitu,ile sehemu tegemeo. Kusema ya kwamba Yesu ni jiwe kuu la pembeni la kanisa ni kusema kwamba hakuna kitu ndani ya kanisa kilicho na umuhimu kuliko Yesu na ya kwamba kila kitu ndani ya kanisa kinamtegemea, (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith)

Sehemu zingine zenye utata katika tafsiri ya sura hii.

Jina

"Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo" (Matendo 4:12). Kwa maneno haya Petro alimaanisha kwamba hamna mtu yeyote ambaye amewahi kuwa duniani ama atakayekuja duniani kuwaokoa watu.

<< | >>

Acts 4:1

Sentensi unganishi

Viongozi wa dini walimkamata Petro na Yohana baada ya Petro kumponya yule mtu aliyezaliwa kiwete.

wakaja kwao

"waliwasogelea" au "walikuja kwao"

Walikuwa wameudhika sana

Walikuwa na hasira. Masadukayo kwa upekee wao wangekuwa na hasira kwa Petro na Yohana kwasababu hawakuamini ufufuo.

walikuwa wanawafundisha watu kuhusu Yesu na kutangaza juu ya kufufuka kwake kutoka kwa wafu

Petro na Yohana walikuwa wakisema Mungu angewainua watu kutoka mautini sawa na vile Yesu alivyoinuliwa kutoka miongoni mwa wafu. Petro anazungumzia ufufuo wa Yesu na ufufuo wa watu wote kwa ujumla.

Waliwakamata

Makuhani na mlinzi wa hekalu pamoja na Masadukayo waliwakamata Petro na Yohana.

Kwavile ilikuwa jioni sasa

Ilikuwa tendo la kawaida kutowahoji watu wakati wa usiku.

na idadi ya wanaume waliokuwa wameamini

Hii inamanisha kwa idadi ya wanaume tu, wanawake na watoto walioamini hawakuhesabiwa.

Walikuwa yapata elfu tano

"walikuwa kama elfu tano" au "iliongezeka hadi elfu tano"

Acts 4:5

Sentensi unganishi

Petro na Yohana wanajibu swali wa viongozi bila ya kuwa na woga.

Maelezo ya jumla

Neno "wao" linafafanua juu ya Wayahydi kwa ujumla wao.

Hata ilipofika asubuhi siku iliyofuata, kwamba

Kipengere hiki kilitumika hapa kuonyesha tukio lilipoanzia.

wakuu wao, wazee na waandishi

Hii ni rejea kwa Sanhendrini, mahakama ya wazee wa kiyahudi kilichounganisha makundi haya matatu ya wayahudi.

Yohana, na Alexander

Wanaume hawa wawili walikuwa wajumbe wa familia ya Kuhani mkuu. Huyu siye yule Yohana Mtume.

Kwa nguvu gani

"nani aliyewapa nguvu" au "kitu gani kiliwapa nguvu." Walijua Petro na Yohana wasingemponya mtu kwa nguvu zao wenyewe.

Kwa jina gani

"ni nani aliyewapa mamlaka"

Acts 4:8

Kisha, Petro, akiwa amejaa Roho Mtakatifu

Roho Mtakatifu akiwa amemjaza Petro.

kama sisi siku ya leo tunahojiwa kuhusu tendo jema lililofanywa kwa mtu huyu mgonjwa - kwa namna gani mtu huyu alifanywa mzima?

Petro aliuliza swali hili kufafanua kwamba ilikuwa sababu halisi ya kuteswa kwao. Mnatuuliza leo kwa namna gani mtu huyu amepata kupona.

Hebu lijulikane hilo kwenu na kwa watu wote katika Israel

Na ijulikane kwenu na watu wote wa Israel kujua hili.

kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti,

Neno "Jina" linafafanua nguvu na mamlaka ya jina hilo. Kwa mamlaka ya Jina la Yesu Kristo wa Nazarethi.

Acts 4:11

Sentensi unganishi

Petro anahitimisha hotuba yake kwa viongozi wa dini ya kiyahudi aliyoianza

Yesu Kristo ni jiwe ambalo ninyi wajenzi mlilidharau, lakini ambalo limefanywa kuwa jiwe kuu la pembeni.

Petro ananukuu kutoka Zaburi, akimaanisha viongozi wa Kiyahudi, kama wajenzi, waliomkataa na Yesu, lakini Mungu alimfanya kuwa wa muhimu zaidi katika ufalme wake, kama jiwe la pembeni katika ujenzi lilivyo la muhimu.

ninyi wajenzi mlilidharau

"Ninyi wajenzi mlimkataa"

Hakuna wokovu katika mtu mwingine awaye yote

Yesu ni mtu pekee aliye na uwezo wa kuokoa

Kwa maana hakuna jina jingine chini ya mbingu walilopewa watu

Hii inamaanisha, hakuna Jina jingine chini ya mbingu Mungu amswapa wanadamu.

ambalo kwa hilo tunaweza kuokolewa.

J"ina ambalo laweza kuokoa au ambaye aweza kuokoa"

Acts 4:13

Maelezo ya jumla

Paulo anaendelea kuzungumzia Wayahudi Viongozi.

Wakati walipoona ujasiri wa Petro na Yohana

Neno "Ujasiri" linaelezea njia ambayo Petro na Yohana wameitumia kujibu za viongozi Wayahudi.

wakagundua kwamba walikuwa ni watu wakawaida wasio na elimu

Wayahudi viuongozi walitambua hivi kwasababu ya njia ambayo Petro na Yohana waliinena.

Walikuwa ni watu wa kawaida, wasio na elimu

Neno "kawaida" na "wasio na Elimu" ni maneno yanayogawana maana moja. Petro na Yohana hawakupata mafunzo ya elimu katika sheria ya kiyahudi

mtu aliyeponywa

Mtu ambaye alikuwa ameponya na Yesu kupitia Petro na Yohana

hawakuwa na kitu cha kusema dhidi ya hili.

Hawakuwa na cha kusema dhidi ya Petro na Yohana juu ya kuponywa kwa huyo.

Acts 4:15

Mitume

Linaelezea juu ya Petro na Yohana.

tutawafanyaje watu hawa?

Wayahudi viongozi wanauliza swali kama wamechanganyikiwa kwasababu kwa kuwa hawakufikiri nini cha kuwatendea Petro na Yohana. "Hakuna cha kuwatendea hawa wanaume"

Ni kweli kwamba muujiza wa ajabu umefanyika kupitia wao unajulikana na kila mmoja anayeishi Yerusalemu

Inamaanisha; kila mtu anayekaa Yerusalamu anajua juu ya muujiza uliotendwa na hawa wanaume.

ili kwamba jambo hili lisienee miongoni mwa watu

Neno "jambo" linamaanisha muujiza wowote au mafundisho ya Petro na Yohana yanaweza kuendelea kusambaa.

kamwe wasinene wala kufundisha kwa jina la hili.

Neno "Jina" linamaanisha ubinadamu wa Yesu. Wasinene tena kwa yeyote kuhusu huyu mtu, Yesu.

Acts 4:19

Maelezo ya jumla

Neno "sisi" linaelezea Petro na Yohana, lakini si kwa wale ambao waliokuwa wakiwaelezea.

Kama ni sahihi machoni pa Mungu

Neno "machoni pa Mungu" linamaanisha maoni ya Mungu. Kama Mungu anafikiri ni sawa kuwatii watu kuliko Mungu.

hatuwezi kuacha kuyanena

"Lazima tutaendelea kunena" au "Hatutaacha kunena"

Acts 4:21

Maelezo ya jumla

Msitari wa 22 unatoa habari ya nyumba kuhusu umri wa mtu kiwete aliyeponywa.

Baada ya maonyo zaidi

Wayahudi Viongozi waliwatishia Petro na Yohana kuwapa adhabu tena.

Hawakuweza kupata sababu yoyote ya kuwaadhibu

Viongozi hawakuweza kupata kujua kwa namna gani wawaadhibu Petro na Yohana bila ya kusababisha vurugu miongoni mwa watu waliomwona mtu aliyeponywa.

kwa kile kilichokuwa kimetendeka

Kwa kile Petro na Yohana walichokuwa wametenda

Mtu aliyekuwa amepokea muujiza wa uponyaji

Mtu yule ambaye Petro na Yohana walikuwa wamemtendea muujiza wa uponyaji.

Acts 4:23

Maelezo ya jumla

Wakinena pamoja, watu walinukuu Zaburi ya Daudi kutoka Agano la Kale.

Maelezo ya jumla

Neno "wao" linamaanisha baadhi ya waumini, lakini si Petro na Yohana.

Walikuja kwa watu wao

Walikwenda kwa waumini wenzao.

kwa Roho Mtakatifu, kwa kinywa cha baba yetu Daudi, mtumishi wako, ulisema

Hii inamaanisha Roho Mtakatifu alisababisha Daudi kunena au kuandika kile Mungu alichosema.

Kwa kinywa cha baba yetu Daudi

Neno "kinywa" linaelezea yale maneno ambayo Daudi aliyasema ama aliyaandika "Kwa maneno ya baba yetu Daudi"

Kwanini watu wa mataifa wamefanya ghasia, na watu wametafakari mambo yasiyofaa?

Hili ni swali lenye jibu linaloelezea maneno yenye ubatili ya kumpinga Mungu.

watu wametafakari mambo yasiyofaa

Watu wanatafakari maneno ya ubatili yaliyo kinyume na Mungu.

Acts 4:26

Sentensi unganiishi:

Waumini wanakamilisha nukuu yao kutoka kwa mfalme Daudi katika zaburi walizozianza

Wafalme wa dunia wamejipanga pamoja, na watawala wamekusanyika kwa pamoja dhidi ya Bwana

Mistari hii miwili, Wafalme na Watawala kimsingi ni jambo moja kuonyesha unganiko la kufanya biidi katika kupinga kazi ya Mungu

wamekusanyika kwa pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya masihi wake

Waliunganisha majeshi yao pamoja kupigana vitani. Au kuwa kinyume na Masihi wa Mungu.

Acts 4:27

Sentensi unganishi

Waumini wanaendelea na maombi.

Katika mji huu

"Katika Yerusalemu"

mtumishi wako mtakatifu Yesu

"Yesu anayekutumikia kwa uaminifu"

kufanya yote ambayo mkono wako na mapenzi yako yaliyaamuru

Neno "Mkono" limetumika kwa maana ya nguvu za Mungu.

Acts 4:29

Maelezo unganishi

Waumini wanakamilisha maombi yao waliyoyaanza

yaangalie matisho yao,

Neno, "Yaangalie" Ni ombi kwa Mungu kuchukua hatua dhidi ya vitisho vya Wayahydi viongozi kwa vitisho vyao kwa waumini.

kwamba unaponyosha mkono wako kuponya

Neno "Mkono" unaelezea nguvu za Mungu katika kuponya watu.

kupitia jina la mtumishi wako mtakatifu Yesu

Neno "Jina" Linamaanisha nguvu na mamlaka ya Mtakatifu Yesu

eneo ambalo walikusanyika kwa pamoja likatikiswa

Eneo walipokuwa wakifanyia maombi pakatikisika.

na wote wakajazwa na Roho Mtakatifu

Roho Mtakatifu aliwajaza wote, na kuanz kulinena neno la Mungu kwa ujasiri

Acts 4:32

Walioamini walikuwa na moyo mmoja na roho moja

Neno "Moyo" linaelezea mawazo kuwa wote waliwaza kitu kimoja na moyo mmoja.

walikuwa na vitu vyote shirika

Waligawana vitu vyao kila mmoja na mwenzake.

na neema kubwa ilikuwa juu yao wote.

Pengine maana yake 1) Mungu aliwabariki waumini zaidi; au 2) Watu katka Yerusalemu waliwasaidia waumini katika hali ya juu.

Acts 4:34

waliokuwa na hati za viwanja au nyumba

Umiliki wa hati za viwanja na nyumba kwa waliokuwa wanamiliki Yerusalemu

waliviuza na kuleta pesa ya vitu waliyokuwa wameuza

Fedha ambayo walilipwa kutoka vitu walivyoviuza.

Waliweka chini ya miguu ya mitume

Hii ilikuwa ni njia ya waumini: 1) kuonyesha waziwazi mabadiliko ya mioyo na 2) kuwapa mitume mamlaka juu ya namna zawadi inavyopaswa kutumika.

mgawanyo ulifanywa kwa kila muumini, kulingana na kila mmoja alivyokuwa na hitaji.

Waligawanya pesa kwa waumini kwa aliyekuwa na uhitaji

Acts 4:36

Maelezo ya jumla

Luka anamwelezea historia ya Barnaba

Yusufu, mlawi, mtu kutoka Kipro, alipewa jina la Barnabasi na mitume

Mitume walimpa Yusufu jina jingine Barnaba

hiyo ikitafasiriwa

ambalo linaweza kupewa tafasiri

mwana wa faraja

Mitume walitumia hivyo kuonyesha kwamba Yusufu alikuwa mtu wa kutia moyo wengine

akaziweka chini ya miguu ya mitume

Aliwasilisha pesa kwa mitume.

Acts 5

Matendo 5 Maelezo kwa jumla

Dhana maalum katika sura hii

"Shetani amekujaza moyo wako kumwambia uongo Roho Mtakatifu"

Hakuna anayejua kwa ukamilifu iwapo Anania na Safira walikuwa Wakristo wa ukweli walipoamua kudangaya kuhusu kipande cha ardhi walichokiuza (Matendo 5:1-10), kwa maana Luka hataji swala hili. Anasema tu kwamba walikuwa "miongoni mwa walioamini" (Luke 4:32).Hata hivyo, Petero alifahamu kwamba walidanganya waumini, na alijua kwamba walikuwa wamsikiliza na kumtii shetani.

Walipowadanganya waumini, pia walimdanganya Roho Mtakatifu kwa sababu anaishi ndani ya Waumini.

Gereza

"Gereza ya uma" ambamo Baraza la Wayahudi walimueka ndani Petero (Matendo 5:18) huenda lilikuwa gereza.

<< | >>

Acts 5:1

Sentensi unganishi

Maelezo ya namna wakristo walivyokuwa wakishirikiana mahitaji kwa baadhi ya wakristo kuuza mali zao. Luka anatuambia habari za waumini wawili Anania na Safira walivyohusika katika ushirika huo.

Sasa

"Lakini sasa." Hii inaonyesha sehemu kumalizika na kuanza kwa maelezo ama habari mpya.

Mke wake pia alilijua

"Mke wake pia alijua kuwa Mmewe alikuwa ametunza nyumbani sehemu ya fedha kwa mauzo ya shamba lao".

kuiweka kwenye miguu ya mitume.

Inamaanisha kwamba waliwasilisha hiyo fedha kwa mitume.

Acts 5:3

Maelezo ya jumla

Kama lugha yako unayotumia haina haitumii maswali yenye majibu ndani ya swali, unaweza kutumia kame sentensi tu.

Kwanini Shetani ameujaza moyo wako...ardhi?

Petro alitumia swali hili kumkemea Anania. "Kwa namna gani umemruhusu Shetani kukushawishi ili kudanganya juu ya kiasi cha mauzo ya ardhi yenu."

kusema uongo kwa Roho Mtakatifu na kuficha sehemu ya mali ya shamba

Inaonyesha Anania alikuwa amewaambia mitume kuwa alichotoa kilikuwa kiasi chote cha mauzo ya shamba lake

Wakati lilipokuwa halijauzwa, halikuwa ni mali yako?

Petro alitumia maswali haya kumkumbusha Anania kwamba alikuwa na uwezo juu ya pesa yake. "Alikuwa na wajibu wa kusimamia pesa yake kwa uadilifu."

Ilikuwaje uwaze jambo hili moyoni mwako?

Petro alitumia swali hili kumkemea Anania. "Hukupaswa kuamua kuwa mwongo juu ya jambo hili."

Anania alidondoka chini na akakata roho

Anania alianguka chini kwasababu alikufa. Hakufa kwasababu alianguka chini bali alikufa na kisha akaanguka chini.

Acts 5:7

mke wake aliingia ndani

Mke wa Anania naye aliingia ndani ya nyumba walimokuwa mitume.

Kilichokuwa kimetokea

"Kwamba mme wake alikuwa amekufa"

kwa thamani hiyo

"Kwa thamani hiyo" linalenga kuthibitisha kama Anania alileta fedha kwa mitume yenye thamani sawa na thamani ya shamba lililouzwa.

Acts 5:9

Sentensi unganishi:

Huu ni mwisho wa sehemu ya habari kuhusu Anania na Safira.

Inakuwaje kwamba mmepatana kwa pamoja kumjaribu Roho wa Bwana?

Petro aliuliza hili kuonyesha hawa wawili kwamba walikubaliana kutenda dhambi kwa pamoja. "Mmekubaliana kwa pamoja kumjaribu Roho!"

miguu ya wale waliomzika mme wako

Hapa "Miguu" inamaanisha wanaume waliomzika Anania.

akadondoka miguuni pa Petro

Inamaanisha Safira alipokufa alidondoka mbele yamiguu ya Petro

Akapumua pumzi ya mwisho

Hii ni namna ya kusema kwamba "alikufa."

Acts 5:12

Sentensi unganishi

Luka anaendelea kuwaambia wasomaji kile kilichotokea siku za mwanzoni mwa kanisa Yerusalemu.

Ishara nyingi na maajabu vilikuwa vinatokea miongoni mwa watu kupitia mikono ya mitume

Miujiza na ajabu nyingi ilitendwa miongoni mwa watu kupitia mikono ya mitume.

ukumbi wa Sulemani.

Hili lilikuwa ni eneo Njia ya kutembea lililokuwa limezungukwa na nguzo zilizojengwa kushikilia paa ambalo watu waliliita Mfalme Sulemani.

walipewa heshima ya juu na watu.

Watu waliwaonyesha waumini heshima ya juu.

Acts 5:14

Maelezo ya jumla

Luka anatoa maelezo juu ya watu waliokuwa wakiishi Yerusalemu

waamini wengi walikuwa wakiongezeka kwa Bwana

Watu wengi walikuwa wakimwamini Bwana.

ili kwamba Petro akiwa anapita, kivuli chake kiweze kushuka juu yao

Inamaanisha kuwa Mungu angeweza kuwaponya wagonjwa kama kivuli cha Petro kingewagusa.

wote waliopagawa na roho wachafu,

"Wale ambao roho wachafu walikuwa wamewapagaa. Waliokuwa wakiteswa na roho wachafu"

wote waliponywa.

Mungu aliwaponya wote kwa njia ya mitume

Acts 5:17

Sentensi unganishi

Viongozi wa dini walianza kuwatesa waumini

Lakini

Neno "lakini" linaanzisha habari kinzani. Unaweza kutafasiri hii kwa namna ambavyo lugha yako hutambulisha habari kinzani.

kuhani mkuu aliinuka,

Neno "kuinuka" linamaanisha Kuhani mkuu aliamua kuchukua hatua, si kwamba aliinuka tu kutoka kwenye kiti chake alichokikalia.

na walijawa na wivu

Inamaanisha walijawa na wivu sana

wakanyosha mikono yao kuwakamata mitume

Waliwakamata mitume kwa nguvu, kwa kuwa walikuwa wameagiza walinzi wao wapate kuwakamata mitume.

Acts 5:19

Nendeni, mkasimame hekaluni

Mitume walikwenda kusimama hekaluni katika ile sehemu ya wazi, hawakuingia ndani ambamo hawaruhusiwi kuingia ispokuwa kwa makuhani tu.

maneno yote ya Uzima huu.

Hii inamaanisha ujumbe wa Injili ambao mitume walikuwa wakiutangaza.

wakati wa kupambazuka

Ilipoanza kuwa nuru, "Ingawa malaika alikuwa amewatoa mitume jela wakati wa usiku, hivyo kulipoanza kupambazuka mitume walikuwa tayari wamefika hekaluni.

kuwatuma gerezani ili kuwaleta mitume.

Inamaanisha kuhani alituma mmoja wao kwenda gerezani kuwachukua mitume na kuwaleta mbele ya baraza.

Acts 5:22

lakini tulipokuwa tukifungua, hatukuona mtu ndani

eno "hatukuona mtu" linawakilisha Mitume kwamba hawakuwakuta wakiwa ndani ya gereza.

Acts 5:24

Walishikwa na butwaa

"walishtushwa" au "walichanganyikiwa"

Kuhusu wao

"kuhusu maneno waliyokuwa wamesikia" (taarifa kwamba mitume hawakuwa katika gereza)

litakuwaje jambo hili

Nini kimefanyika hata watu hawa kutoka nje alihali milango imefungwa na walinzi wakiwepo.

wamesimama hekaluni

Mitume hawakuwa ndani ya hekalu wanamoruhusiwa kiungia makuhani tu, bali walikuwa wamesimama kwenye ukumbi wa nje wa hekalu.

Acts 5:26

Sentensi unganishi

Mlinzi na maafisa waliwaleta mitume mbele ya baraza la viongozi wa dini.

waliwaogopa watu

Mitume walipelekwa bila vurugu mbele ya baraza, viongozi walikuwa wamewahofia watu juu ya kitendo chochote wangekifanya kwa mitume.

Katika jina hili

Neno "Jina" linamaanisha Yesu Kristo. Mitume walizuiliwa wasinene neno lolote kupitia Jina la Yesu.

mmeijaza Yerusalemu kwa fundisho lenu

Inamaanisha wamewafundisha watu wote wa Yerusalemu habari za Yesu.

na kutamani kuleta damu ya mtu huyu juu yetu.

Neno "Damu" linamaanisa kifo cha Yesu na damu yake. Kwamba Viongozi hao walipaswa kuwajibika kwa kuhusika kwao kumwua Yesu Kristo.

Acts 5:29

Petro na mitume wakajibu

Petro alizungumza kwa niaba ya mitume wote kwa maneno yafuatayo.

kwa kumtundika juu ya mti

Petro anatumia neno "mti" kuonyesha kuwa msalaba ulitengenezwa kutokana na mti. "Kwa kumtundika juu ya msalaba"

kutoa toba kwa Israeli, na msamaha wa dhambi

Neno "toba" na "msamaha" yanamaanisha kuleta msamaha kwa watu wa Israeli kwa njia ya toba na kisha Mungu kuwasamehe dhambi zao.

Israeli

Linamaanisha Wayahudi wote.

kwa wale wanaomtii

"Wote wanaojikabidhi chini ya mamlaka ya Mungu"

Acts 5:33

Sentensi unganishi

Gamalieli anatoa maelezo mbele ya wajumbe wa baraza

Gamalieli, mwalimu wa sheria, aliyeheshimiwa na watu wote

Luka anamwelezea Gamarieli juu ya historia yake.

aliyeheshimiwa na watu wote

Alikuwa anaheshimiwa na watu wote

alisimama na kuwaamuru mitume wachukuliwe nje

Gamalieli aliwaagiza walinzi wawatoe nje mitume kwa muda.

Acts 5:35

Wanaume wa Israeli, iweni makini sana na kile mnachopendekeza kuwafanyia watu hawa

Gamarieli anawaeleza majumbe wa baraza wasifanye jambo lolote juu ya hao mitume litakalowaletea majuto baadaye

Theuda aliinuka na kujidai kuwa mtu mkuu

Theuda alikuwa ameasi na kujitwalia idadi kubwa ya wafuasi

Aliuawa, na wote waliokuwa wanamtii walitawanyika

Watu walimwua na jamii ikatawanyika.

Baada ya mtu huyu, Yuda mgalilaya, aliinuka siku zile za kuandikwa sensa, akavuta watu wengi nyuma yake.

Yuda Mgalilaya naye vilevile alitokea wakati wa sensa ya Kaisari, aliwavuta wengi kuasi dhidi ya utawala wa dola ya Kirumi kisha naye kapotea.

Acts 5:38

Sentensi unganishi:

Gamarieli anamaliza kuwaeleza wajumbe wa baraza. Pamoja na kuwapiga wale mitume na kuwaamuru wasizidi kunena habari za Yesu na kuwaachia huru, lakini wanafunzi walizidi kufundisha na kuhubiri habari za Yesu.

jiepusheni na watu hawa na muwaache wenyewe,

Gamalieli anawaambia Wayahudi viongozi wasiwaadhibu hao mitume na wasiwatie tena gerezani.

kama mpango huu au kazi hii ni ya watu itatupwa

Kama jambo hili wanalolitenda chimbuko lake ni mwanadamu litakoma tu.

Lakini kama ni ya Mungu, hamtaweza kuwazuia

Kama kazi hii wanayoifanya chimbuko lake ni Mungu, kazi hii itaendelea.

Hivyo, walishawishika na maneno yake.

Gamalieli alifanikiwa kuwashawishi Viongozi Wayahudi na kukubaliana na ushawishi wake.

Acts 5:40

Kisha, waliwaita mitume ndani na kuwachapa

Wajumbe wa baraza waliwaamru walinzi wa hekalu kuwachapa viboko mitume.

kuwaamuru wasinene kwa jina la Yesu

Wasinene tena juu ya jina la Yesu lenye mamlaka.

wamehesabiwa kuwa wamestahili kuteseka na kutoheshimiwa kwa ajili ya Jina hilo

Ilikuwa ni faida kuteswa na kudharauliwa kwa ajili ya Yesu.

Baada ya hapo kila siku

"Baada ya siku hiyo, kila siku." Kifungu hiki kinaonyesha kile walichokifanya mitume kila siku kwa siku zilizofuata. Walitiwa moyo kufanya hili kwasababu ya kile kilichotokea katika tukio hilo la kuadhibiwa kwao.

Waliendelea kufundisha

"Hawakuacha kufundisha" Hekaluni na katika nyumba za waumini.

Acts 6

Matendo 06 Maelezo kwa jumla

Dhana maalum katika sura hii

Mgao kwa wajane

Waumini wa Yerusalemu waliwapa wajane chakula kila siku. Wote walikuzwa kama Wayahudi ingawa wengine wao walikua wameishi Yudea na walizungumza Kihebrania, na wengine walikuwa wameishi kwa Mataifa na walizungumza Kigiriki. Waliogawa chakula walikigawa kwa wajane waliozungumza Kihebrania na kuwaacha wale ambao hawakukizungumza. Kumfurahisha Mungu, viongozi wa kanisa waliwateua wanaume waliokifahamu Kigiriki kwa kugawa sehemu ya chakula kwa wajane waliokifahamu Kigiriki Mmoja wa" hao wanaume alikuwa Stefano.

Utata mwingine katika tafsiri ya sura hii

"Uso wake ulikuwa kama wa malaika"

Hakuna ajuaye vile uso wa Stefano ulivyokuwa kama uso wa malaika kwa maana Luka hatuambii hilo. Ni vema tafsiri hii kusema tu kuhusu kinachosema ULB kuhusu haya.

<< | >>

Acts 6:1

Maelezo ya jumla:

Huu ni mwanzo wa sehemu mpya ya habari. Luka anatoa habari muhimu ya kuweza kujifunza.

Sasa katika siku hizi

Hii inaonyesha mwanzo wa sehemu mpya ya habari. Zingatia namna ambavyo sehemu mpya ya habari zinavyotambulishwa katika lugha yako.

Kuongezeka

"Kuongezeka kukubwa"

Wayahudi wa Kiyunani

Hawa walikuwa ni wayahudi ambao walikuwa wakiishi maisha yao zaidi sehemu fulani katika utawala wa kirumi nje ya Israel, na walikuwa wakiongea Kigiriki. Lugha na utamaduni wao vilikuwa kidogo tofauti na wale waliokulia Israeli.

Wahebrania

Hawa walikuwa ni wayahudi waliokuwa wamekulia Israel wakiongea Kiaramaiki. Kanisa liliwaangalia tu wayahudi na wafuasi wa kiyahudi mpaka hapo.

Wajane

Mjane wa kweli alikuwa ni mwanamke ambaye mme wake alikuwa amekufa, na hakuna jamaa wowote wa kumtunza.

wajane wao walikuwa wanasahaulika

"kupuuzwa" au "kusahaulika." Kulikuwa na wengi sana waliohitaji msaada kiasi kwamba baadhi walikoswa hasa Wayahudi wa Kiyunani.

Mgawanyo wa kila siku wa chakula

Pesa ambayo ilitolewa kwa mitume ilitumika kwa sehemu kununua chakula kwa ajili ya wajane wa kanisa la kwanza.

Acts 6:2

Mitume kumi na wawili

Hapa wanazungumziwa mitume kumi na moja pamoja na Mathias aliyekuwa amechaguliwa.

kusanyiko lote la wanafunzi

"Wanafunzi wote" au "Waumini wote"

Siyo sahihi kwetu kuliacha neno la Mungu

Ni neno lenye msisitizo wa muhimu wa kutokuacha huduma ya kufundisha neno la Mungu

Kuhudumia meza

Hili ni neno kwa ajili ya kuhudumia chakula kwa watu.

Wanaume wema, waliojawa na Roho na hekima

Uwezekano wa maana waweza kuwa 1) Wanaume wana sifa tatu- wema, kujazwa na Roho, na kujazwa na hekima au 2) wanaume wana tabia njema kwa sifa mbili- kujazwa na Roho, na kujawa na hekima.

kuwakabidhi huduma hii.

Kuwa na wajibu kwa huduma hiyo muhimu.

huduma ya neno

Ni huduma ya kufundisha na kuhubiri habari njema.

Acts 6:5

Hotuba yao ikaupendeza mkutano wote

Hotuba yao ilikubaliwa, pendekezo lilikubaliwa na jamii yote ya waumini.

Stefano...na Nikolao

Haya ni majina ya kigiriki, na mapendekezo yalikuwa kwamba wanaume walioteuliwa walikuwa zaidi au wote kutoka kundi la waumini wa wayahudi wa kigiriki.

Mwongofu

"Mtu wa mataifa aliyeamini dini ya kiyahudi"

Waliweka mikono yao juu yao

Kuwapa baraka na kuwakabidhi wajibu na mamlaka kwa kazi ya watu saba

Acts 6:7

Maelezo ya jumla:

Msitari huu ni neno linalotoa taarifa mpya juu ya ukuaji wa kanisa.

Neno la Mungu liliongezeka

Idadi ya watu walioliamini neno la Mungu iliendelea kuongezeka. hivyo kwa lugha nyingine neo la Mungu liliongezeka.

Wakawa watii kwa imani

"Walikubali kuifuata njia mpya ya imani"

Imani

Hii inaweza kuwa; 1) Ujumbe wa Injili wa matumaini katika Yesu; au 2) Mafundisho ya kanisa; au 3) Mafundisho ya kikristo.

Acts 6:8

Sentensi unganishi

Huu ni mwanzo wa sehemu mpya ya hadithi.

Maelezo ya jumla

Mistari hii inatupa maelezo ambayo Stefano na watu wengine hali ilivyoendelea kuwa.

Na Stefano

Luka anamwelezea Stefano kama kinara wa sehemu ya simulizi hii.

Stefano, aliyejaa neema na nguvu, alikuwa akifanya

Neno "Neema" na "Nguvu" yanaelezea nguvu kutoka kwa Mungu. Yaani Mungu alikuwa akimpa nguvu Stefano za kutenda.

Sinagogi la Mahuru

"Mahuru" walikuwa yumkini watumwa huru kutoka sehemu hizi tofautitofauti. Haijulikani kama watu wengine walioorodheshwa walikuwa sehemu ya Sinagogi au walishiriki tu katika mdahalo na Stefano.

Kufanya mdahalo na Stefano

"kubishana na Stefano" au "kujadiliana na Stefano"

Acts 6:10

Sentensi unganishi:

Taarifa za nyuma zilizoanza zinaendelea katika mstari wa 10.

Hawakuweza kushindana

"Wasingeweza kuthibitisha uongo kwa kile Stefano alichosema"

Waliwashawishi kwa siri

Kwa kuwa jambo lilifanywa kwa siri, inathibitisha kwamba ushuhuda wao ulikuwa wa uongo.

Maneno ya kukufuru

"maneno kinyume na sheria ya Mungu na Musa"

Acts 6:12

Kuwashurutisha watu

"kuwahamasisha watu kwa kiwango cha kuwa na hasira"

na kumwendea Stefano

Kisha wote wakamwendea kwa nguvu

Kumkamata

"kumshika kwa nguvu"

mtu huyu haachi kunena

anaendelea kunena mara zote.

Kila mmoja aliyekuwa katika baraza, akaelekeza macho yake kumwangalia Stefano

"kuangalia kwa shauku kwake." Hii ni msemo ukimaanisha kuelekeza macho kwake."

Alikuwa kama uso wa malaika

Hii ni tabasamu kama kulinganisha na kiwango cha mfanano unaofanana na kuwa "mng'ao" ambao haujasemwa. "alikuwa anang'aa kama uso wa malaika"

Acts 7

Matendo 07 Maelezo kwa Jumla

Muundo na Mpangilio

Tafsiri zingine zimeweka kila mstari wa ushairi mbele ya kulia kuliko maandishi mengine ili kurahisisha kusoma. ULB hufanya hivi na ushairi ambao umenukuliwa kutoka Agano la Kale 7:42-43 na 49-50.

Inaonekana kwamba 8:1 ni sehemu ya utungo wa sura hii.

Dhana maalum katika sura hii

"Stefano alisema"

Stefano alihadithia historia ya Israeli kwa ufupi. Alisisitiza ule muda Wana wa Israeli walikuwa wamewakataa watu Mungu alikuwa amechagua kuwaongoza. Mwisho wa habari, alisema viongozi wa Wayahudi aliokuwa akiwazungumzia walikuwa wamemkataa Yesu jinsi Waisraeli watenda dhambi walikuwa wakiwakataa viongozi walioteuliwa na Mungu.

"Jazwa na Roho Mtakatifu"

Roho Mtakatifu alimwongoza Stefano kana kwamba alisema tu kile Mungu alitaka aseme.

Kuashiria yajayo

Mwandishi anapolizungumzia jambo ambalo si muhimu kwa wakati huo lakini litakuja kuwa muhimu baadaye katoka hadithi hiyo, hii huitwa kuashiria yajayo. Luka anamtaja Saulo, aliyejulikana kama Paulo kwa hii hadithi ingawa si mhusika wa maana kwenye habari hii. Hii ni kwa maana Paulo ni mtu muhimu katika sehemu zilizobaki kwenye hiki kitabu cha Matendo ya Mitume.

Mifano muhimu za usemi katika Sura hii

Mawasiliano yaliyolengwa

Stefano alikuwa akizungumza na Wayahudi walizifahamu vyema sheria za Musa na kwa hivyo hakufafanua vitu ambavyo wasikilizaji wake walikuwa wanajua mbele. Lakini utahitajika kueleza baadhi ya vitu hivi ili wasomi wako waweze kuelewa alichokuwa anasema Stefano. Kwa mfano labda utaeleza vizuri kwamba wakati ndugu zake Yusufu "walimuuza Misri" (Matendo 7:9), Yosufu alikuwa anaenda kuwa mtumwa Misri, (tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metonymy)

Metonymy

Stefano alizungumzia Yusufu kuongoza "Juu ya Misri" na juu ya nyumba ya Farao. Hapa alimaanisha ya kwamba Yusufu aliongoza watu wa Misri na watu na mali yote iliyokuwa ndani ya nyumba ya Farao (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metonymy).

Matatizo mengine ya tafsiri katika sura hii

Maelezo ya awali

Viongozi wa Wayahudi ambao Stefano aliwazungumzuia walikuwa wanafahamu mbele matukio aliyokuwa akiwazungumzuia. Walifahamu kwamba Musa aliandika Kitabu cha Mwanzo. Kama kitabu cha mwanzo hakikutafsiriwa katika lugha yako, itakuwa vigumu kwa wasomaji wako kuelewa alichosema Stefano.

<< | >>

Acts 7:1

Sentensi unganishi

Sehemu ya habari kuhusu Stefano iliyoanzia sura 6:8 inaendelea. Stefano anaanza kumjibu Kuhani Mkuu na baraza kwa kuanza kuzungumzia mambo yaliyotukia katika historia ya Israeli. Maelezo mengi ya Stefano yanatoka kwenye vitabu vya sheria vya Musa.

Maelezo ya ujumla

Kwenye mstari wa 2,Stefano anaanza hotuba yake kumjibu kuhani mkuu na baraza.Anaanza hotuba yake kwa kuongelea mambo yaliyotokea katika historia ya Israeli.

Ndugu na baba zangu,nisikilizeni mimi.

Stefano alikuwa akiheshimika sana kwenye baraza kwa salamu yake ya kifamilia.

Acts 7:4

Hakumpa chochote kama urithi wake

Hakuweza kutoa chochote katika hiyo.

hapakuwa na sehemu hata ya kuweka mguu

Inaweza kuwa na maana ya; 1) Eneo pana la kuweza kusimama; au 2) Aridhi ya kutosha kuweza kutembea kwa hatua kadhaa.

kama miliki yake na uzao wake

Kwamba nchi itakuwa mali yake milele yeye na uzao wake.

Acts 7:6

Mungu alinena naye hivi

Badaaye Mungu alimwambia Ibrahimu.

miaka mia nne.

Miaka mia nne (400).

nitalihukumu taifa

Neno "taifa" linamaanisha watu walio ndani yake. Mungu atawahukumu watu wa taifa.

ambalo litawafanya mateka

Nchi ambayo uzao wako watakuwa mateka.

akampa Abrahamu agano la tohara

Mungu alifanya Agano na Abrahamu la tohara kwa watoto wake wote wa kiume.

Abrahamu akawa baba wa Isaka

Ni habari inayoelezea Uzao wa Abrahamu.

na Yakobo akawa baba

Na Yakobo akawa baba, Stefana anaelezea kwa ufupi.

Acts 7:9

Mababu

Wana wakubwa wa Yakobo " "au" ndugu wakubwa wa Yusufu"

wakamwonea wivu Yusufu

Ndugu zake wakubwa na Yusufu walijawa na wivu dhidi yake.

wakamuuza katika nchi ya Misri

Wayahudi walijua kuwa mababu zao walimwuza Yusufu na kuwa mtumwa katika nchi ya Misri.

Na Mungu

Inafaa kutumika kiuhalisia kuwa; "lakini Mungu" alikuwa pamoja naye huko.

Juu ya Misri

Yusufu akawatawala watu wote wa Misri

na juu ya nyumba yake yote

linaelezea; na kila kitu Farao alichokuwa anakimiliki nyumbani kwake.

Acts 7:11

Kukawa na njaa

"Kukawa na njaa."ardhi ikaacha kutoa chakula

Mababa zetu

"Ndugu zake wakubwa Yusufu"

Nafaka

"Chakula"

aliwatuma baba zetu...Kaka zake

Yakobo aliwatuma baba zetu, ndugu zake na Yusufu.

Katika safari ya pili

Katika safari yao ya pili ya kufuata chakula huko Misri.

Akajionyesha

Yusufu akajifunua kwa ndugu zake na kujitambulisha kama ndugu yao.

familia ya Yusufu ikajulikana kwa Farao.

Kwa maana nyingine; Farao akafahamu kuwa hao walikuwa ndugu zake na Yusufu.

Acts 7:14

Yusufu akawatuma ndugu zake kwenda

liwatuma ndugu zake kwenda Kanaani, nyumbani kwa kaka zake.

Yakobo akafa yeye na baba zetu,

"Yakobo na ndugu zake, baba zetu" wote walikufa.

Wakachukuliwa hata Shekemu wakazikwa

"Uzao wa Yakobo walimchukua na kwenda kumzika katika makaburi walikozikwa ndugu zake.

kwa vipande vya fedha

"kwa fedha"

Acts 7:17

Wakati wa ile ahadi ambayo Mungu alimwahidi Abrahamu ulipokaribia, watu wakiwa wameongezeka huko Misri,

Katika baadhi ya lugha zingine inaweza kuwa msaada ikisomeka; Idadi kubwa ya watu ilipoongezeka, badala ya kusema; muda wa ahadi ulipowadia.

Muda wa ahadi ulipokaribia

Ulikuwa umekaribia muda ambao Mungu angetimiza ahadi yake kwa Ibrahimu.

aliinuka mfalme mwingine

falme mwingine alianza kutawala

Juu ya Misri

"Misri" inasimama badala ya watu wa Misri. "Watu wa Misri"

Nani asiyejua kuhusu Yusufu

"Yusufu"inarejea sifa njema ya Yusufu. "Nani hakujua kuhusu mamlaka ya Yusufu huko Msri."

Waliwatenda mabaya baba zetu.

"Waliwatenda mababu zetu kimaskini"au" "walichukua faida kwa mababu zetu"

Waliwatupa watoto wao wachanga

kuwatupa watoto wao wachanga ili wasiishi

Acts 7:20

Katika kipindi kile Musa alikuwa amezaliwa

Haya ni maelezo ya kumtambulisha mtu mpya, Musa.

Alikuwa mzuri mbele za Mungu

Musa alikuwa kijana mzuri

Akalelewa miezi mitatu

Wazazi wake walimlea Musa miezi mitatu.

Wakati alipotupwa nje

Musa "alitupwa" kwa sababu Farao alikuwa ameamuru kila mtoto wa kiume azaliwapo lazima atupwe. Wazazi wake walilazimika kumweka nje ya nyumba yao.

Binti Farao alimchukua na kumfanya kama mwana wake

kama vile alikuwa mwanaye wa kiume wa kuzaa

Acts 7:22

Musa alifundishwa

"Wamisri walimfundisha Musa"

Mafundisho yote ya kimisri

hii inaongezea ,"vitu vyote walivyovijua Wamisri."

alikuwa na nguvu katika maneno na matendo

"alikuwa na uwezo katika maneno na matendo yake"

ikamjia katika moyo wake

Musa alitafakari na kisha akaamua

kutembelea ndugu zake, Wana wa Israeli

Kuona jinsi gani ndugu zake, wana wa Israeli wanaendeleaje.

Alipomwona Mwisraeli akitendewa mabaya

Alipomwona Mmisri anamtesa mwisraeli, Musa alimtetea na akalipiza kisasi kwa kumpiga hadi kufa yule Mmisri.

Musa alifikiri

" Musa alidhani kuwa, alichokifanya ndugu zake watajua kuwa ni Mungu anawapigania"

kwa mkono wake

kupitia yeye Mungu alikuwa akiwaokoa ndugu zake.

Acts 7:26

baadhi ya Waisraeli

Waisraeli wawili aliwaona wanaogombana wao kwa wao.

akajaribu kuwapatanisha

Alijaribu kuwazuia wasipate kuendelea na ugomvi.

Mabwana, Ninyi ni ndugu;

Musa alikuwa akizungumza na hao waisraeli waliokuwa wakigombana

mbona mnakoseana ninyi kwa ninyi,?

Musa aliuliza swali kuwatia moyo waache kugombana. Msizidi kugombana tena

Nani kakufanya mtawala na mwamuzi wetu?

Hili swali lilitumika kumkemea Musa."Huna mamlaka juu yetu"!

Wewe unataka kuniua , kama ulivyomuua Mmisri jana?"

Mtu yule alitumia swali hilo kumwonya Musa aanze kuzani yawezekana wengi wao walimwona akimwua yule Mmisri.

Acts 7:29

Maelezo ya jumla

Jamii iliyokuwa inamsikiliza Stefani ilikuwa inajua kuwa Musa alikuwa amemwoa mwanamke wa kimidiani alipokimbia kutoka Misri.

Baada ya kusikia haya

Musa alipotambua kuwa Waisraeli wanajua kuwa alikuwa amemwua Mmisri siku moja kabla.

Baada ya miaka arobaini kupita

Wakati miaka arobaini imepita baada ya Musa kutoka Misri.

malaika akamtokea

Stefano alikuwa akiongea na kungi ambalo lilijua pia kuwa Mungu aliongea na Musa kwa njia ya Malaika.

Acts 7:31

alishangaa na kustaajabia kile alichokiona

Musa alishangaa kwamba kichaka hakiungui moto. Hii ilijulikana na watazamaji wa Stefano.

Aliposogelea kwenda kutazama ....Musa alitetemeka na hakuthubutu kuangalia

Hii inamaanisha Musa alikisogelea kichaka kwa karibu ili kuchunguza kilichokuwa kinatokea, lakini ghafla akarudi nyuma kwa hofu aliposikia sauti ikitoka ndani ya kichaka.

Mimi ni Mungu wa baba zako

"Mimi ni Mungu ambaye baba zako waliniabudu"

Musa alitetemeka

Musa alitetemeka kwa hofu.

Acts 7:33

Vua viatu vyako

Mungu alimwambia Musa hivyo ili kumweshimu Mungu.

Sehemu unayosimama ni mahali patakatifu

Musa, eneo unalosimama sasa ni Mungu amelifanya kuwa takatifu, Uwepo wa Mungu ukpo katika eneo hili.

Nimeona

Nimeona kwa hakika pasipo shaka.

Watu wangu

Watu wa Mungu "Uzao wa Abraham,Isaka na Yakobo"

Nimeshuka ili niwaokoe

"nami nimeshuka ili kuwaondolea vifungo"

sasa njoo

"Jiandae" au "KUwa tayari" kwenda. Mungu anatumia amri, anamwamrisha.

Acts 7:35

Maelezo ya jumla

Baada ya Waisraeli kutoka Misri, walikaa miaka 40 wakizunguka zunguka jangwani kabla Mungu hajawaongoza kuingia katika nchi aliyokuwa amewaahidi kuwapa.

Huyu ni Musa ambaye walimkataa

Hii inarejesha nyuma matukio yaliyotunzwa

Nani aliyekufanya mtawala na mwamuzi ?

Hili swali lilitumika kumkemea Musa."Huna mamlaka juu yetu"!

Mtawala na mkombozi

"Kutawala juu yao na kuwaweka huru kutoka kuwa watumwa"

Kwa mkono wa malaika

"Kwa nguvu ya malaika"

Kipindi cha miaka arobaini

"kipindi cha miaka arobaini ambacho watu wa Israeli waliishi jangwani"

Kutoka miongoni mwa ndugu zenu

"kutoka miongoni mwa watu wenu kuwa Nabii"

Acts 7:38

Maelezo ya jumla

Mstari wa 40 ni nukuu kutoka katika vitabu vya sheria vya Musa.

Huyu ni miongoni mwa mtu ambaye alikuwa katika mkutano

"Huyu ni Musa mtu ambaye ni miongoni mwa Waisraeli.

Huyu ni mtu ambaye Mungu aliongea naye maneno yaliyo hai na kutupa sisi

"Huyu ni mtu ambaye Mungu aliongea naye neno lililo hai kutupa sisi"

Neno lililo hai

Maana sahihi ni 1) "ujumbe ambao uliopo" au 2) "maneno yaletayo uzima."

Walimsukuma mbali nao

Mfano huu unaonyesha kukataliwa kwa Musa, "walimkataa yeye kama kiongozi wao"

katika mioyo yao waligeukia Misri

"WAlikusudia kurejea tena Misri"

Wakati huo

"Walipoamua kurudi Misri"

Acts 7:41

Maelezo ya Jumla

Hapa nukuu ya Stefano inatoka kwa Nabii Amosi

Walitengeneza ndama

walitengeneza sanamu mfano wa ndama ili waiabudu.

ndama... hiyo sanamu kazi ya mikono yao

Fungu lote hili linafafanua ndama yule aliyetengenezwa.

Mungu aligeuka

Mungu aligeukia mbali kwa kuwa hakupendezwa na watu hao na kutokuwasaidia tena. Mungu aliacha kuwarekebisha.

Akawaacha

"Akajiondoa kwao

waabudu nyota za angani,

Inaweza kuwa; 1) Nyota pekee au 2) Jua, Mwezi na Nyota.

kwenye kitabu cha manabii

Ni muunganiko wa maandiko kutoka Manabii wa Agano la Kale.

Je mnanitolea mimi sadaka za wanyama mliowachinja .....Israeli

Mungu aliwauliza Waesraeli swali kuonyesha kuwa walikuwa hawamwabudu yeye wala kumtolea dhabihu zao. "Hamkuniheshimu mimi wakati mlipochinja wanyama wasiofaa na kutoa dhabihi .... Israeli".

Nyumba ya Israeli

Hii ni ujumla wa Taifa la Israeli

Acts 7:43

Sentensi unganishi

Stefano anaendeleza majibu yake kwa Kuhani Mkuu na wajumbe wa baraza

Maelezo ya Jumla.

Hii ni nukuu Stefano anaiweka kutoka kwa Nabii Amosi

Mliipokea

Inamaanisha waliitwaa hiyo miungu pamoja nao wakasafiri pamoja nayo huko Jangwani

Hema ya kukutania ya Moleki

Hema ya kukutania au hema ambalo lilijengwa kumwabudu mungu Moleki

Nyota ya mungu Refani

nyota ambayo ilimtambulisha mungu wa uongo Refani

picha ambayo mliitengeneza

Walitengeneza picha ya mungu Moleki na Refani kwa kusudi la kumwabudu.

nitawapeleka mbali zaidi ya Babeli.'

Nitawaondoa kwenye maeneo hata mbali zaidi ya Babeli. Huu ni mwitikio wa hukumu ya Mungu.

Acts 7:44

Hema la kukutania la ushuhuda.

hema ambalo lilijengwa kulifunika sanduku lililokuwa na amri kumi zilizochorwa kwenye mawe na kuwekwa ndani ya sanduku.

Kumiliki Taifa

Hii itajumuisha nchi ,majengo,wanyama na vyote na miliki zote za taifa ambalo Israeli walikuwa wakiwashinda maadui na kuchukua nyara.

Hii Ilikuwa hivi mpaka siku za Daudi

Sanduku la agano lilibaki kwenye hema na ilijumuisha muda wa Daudi, mfalme wa Israeli

Mahali pa makao ya Mungu wa Yakobo

Daudi alitaka sanduku la agano likae Yerusalemu, siyo litangatange kwenye hema kuwazunguka Israeli

Acts 7:47

Maelezo ya jumla

Mistari ya 49-50, Stefano ananukuu maneno kutoka kwa Nabii Isaya. Katika nukuu, Mungu anaongea kuhusu yeye mwenyewe.

zilizojengwa kwa mikono

zilizotengenezwa na watu

Mbinguni ni kiti changu cha enzi ....na duniani ni sehemu ya kuwekea miguu yangu.

Nabii analinganisha ukuu wa Mungu na jinsi isivyowezekana kwa mtu sehemu kwa Bwana kupumzika katika nchi tangu dunia ilipokuwa utupu lakini ni sehemu ya Mungu kuwekea miguu tu.

Ni nyumba ya aina gani mnaweza kunijengea?

Mungu anauliza swali ili kuonesha namna gani mwanadamu ana mapungufu kufikia uumbaji wake. Huwezi kujenga nyumba ambayo itanitosha mimi!

Wapi sehemu yangu ya kupumzikia

Mungu anauliza hili swali kumwonyesha mwanadamu kwamba hawezi kumpatia Mungu mapumziko. "Hakuna sehemu nzuri ya kumtosha Mungu kupumzikia!"

Siyo mikono imefanya haya yote?

Mungu anauliza hili swali kuonyesha kwamba mwanadamu hatengenezi chochote. "Mkono wangu umefanya hivi vitu vyote!

Acts 7:51

Sentensi unganishi

Kwa karipio kali, Stefano anamalizia kumjibu Kuhani Mkuu na baraza kwa staili ile aliyoanza nayo sur 7:1.

Enyi watu wenye shingo ngumu

Shingo ngumu -Stefano alibadilisha kutoka utambulisho wa viongozi wa Kiyahudi na kuwakemea

shingo ngumu

Shingo ngumu -Hii haina maana walikuwa na shingo ngumu, lakini anawaambia kuwa walikuwa wasumbufu.

moyo usiotahiriwa

Moyo usiomtii Mungu. Wayahudi walilitumia neno kwa watu wasio na tohara ni sawa na watu wasiomtii Mungu. Stefano alitumia "moyo' na "masikio" kuwakilisha Wayahudi viongozi waliotenda kwa namna ya watu wa mataifa walivyokuwa wakitenda. Viongozi hawa hawakumtii na wala kumsikiliza Mungu.

Ni manabii wapi baba zenu hawakuwatesa?

Stefano aliuliza swali kuwaonyesha kwamba hakujifunza chochote katika makosa ya baba zao. "Baba zao waliwatesa kila nabii"!

Mmoja mwenye Haki

Anamaanisha juu ya Kristo, Masihi.

mmekuwa wasaliti na wauaji wake pia,

"Mlimsaliti na kumwua"

sheria ile iliyoagizwa na malaika lakini hamkuishika.

"Sheria ambazo Mungu alizituma kwa Malaika kuwaba baba zetu.

Acts 7:54

Sentensi unganishi

Baraza lilimjia juu Stefano kutokana na ujumbe wake.

wajumbe wa baraza waliposikia mambo haya,

Hii ni hatua ya kugeuka; mahubiri yalifikia mwisho na baraza likachukua hatua.

wakachomwa mioyo

Hii ni fumbo kwa, "kujawa na hasira"

wakamsagia meno

Hili ni fumbo linaloelezea hasira nzito au chuki. "walikuwa na hasira ambayo walisaga meno yao kwa pamoja."

Aliangalia mbinguni kwa makini

"Aliangalia juu kwenye mawingu."Inatokea kwamba Stefano peke yake aliona maono siyo mwingine yeyote katika mkutano.

akaon utukufu wa Mungu

Kwa kawaida watu walizoea kuuona utukufu wa Mungu kwa ishara ya nuru." :mwanga mkali kutoka kwa Mungu". Stefano katika maono yake alimwona Mwana wa Adamu amesimama mkono wa kuume wangu.

Mwana wa Adam

Stefano alimtambulisha Yesu kwa cheo cha "Mwana wa Adam."

Acts 7:57

wakaziba masikio yao

Waliziba masikio yao wasiweze kusikia zaidi alichokuwa akisema Stefano.

Nguo za nje

mavazi ya nje au nguo mojawapo walizokuwa wakivaa juu ya nguo zingine.

Wakamtupa nje ya mji

baraza la wazee wakampiga Stefano wakamkamata kwa nguvu na kumtupa nje ya mji

miguuni mwa

"mbele ya "kwa kusudi la kuzilinda

kijana

Sauli alikuwa na umri wa kati ya miaka 30 wakati ule.

Acts 7:59

Sentensi unganishi

Maelezo ya Stefano yanakomea katika sura hii ya 7.

"Pokea roho yangu"

"Chukua Roho yangu" Hili lilikuwa ni ombi toka kwa Stefano.

Akapiga magoti

Hii ni namna ya kuonyesha unyenyekevu kwa Mungu.

usiwahesabie dhambi hii

Inamaanisha; Uwasamehe dhambi hii.

akakata roho

Ni lugha nyingine kuonyesha umauti wa mtu.

Acts 8

Matendo 08 Maelezo ya jumla

Muundo na Mpangilio

Tafsiri zingine zimeweka kila mstari wa ushairi mbele ya kulia kuliko maandishi mengine ili kurahisisha kusoma. ULB hufanya hivi na ushairi ambao umenukuliwa kutoka Agano la Kale 8:32-33

Sentensi ya Kwanza ya mstari wa 1 inaishia na maelezo ya matukio ya sura ya 7: Luka anaanza sehemu mpya ya historia yake na maneno "Hapo ikaanza".

Dhana maalum katika sura hii.

upokea Roho Mtakatifu

Katika sura hii, Luka anawazungumzia kwa mara ya kwanza juu ya watu wanaopokea Roho Mtakatifu (Matendo 8:15-19).Roho Mtakatifu alikuwa mbele amewawezesha waumini kunena kwa lugha, kuwaponya wagonjwa na kuishi kama jumuia na alikuwa amemjaza Stefano pia. Lakini wakati Wayahudi walipoanza kuwafunga waumini katika gereza waumini walioweza kutoroka Yerusalemu walitoroka na walipokuwa wakiondoka waliwahubiria watu kumhusu Yesu. Wakati watu waliosikia ujumbe kuhusu Yesu walipokea Roho Mtakatifu, viongozi wa kanisa walijua kwamba watu hao walikuwa waumini wa ukweli.

Ilitangazwa

Sura hii inazungumzia waumini wakitangaza neno, habari njema na kumtangaza Yesu kwamba ndiye Kristu kuliko sura zingine za kitabo cha Matendo. Neno "tangaza" ni tafsiri ya neno la Kigiriki linalomaanisha kusema habari njema kuhusu jambo ama kitu.

<< | >>

Acts 8:1

Sentensi unganishi

Simlizi inamalizika kumhusu Stefano, kuanzia sura hii ya 8 simlizi inaanza kumtaja Sauli.

siku hiyo ndipo alipoanza... isipokuwa mitume.

Sehemu ya mstari huu wa 1 ni habari inayoeleza kuanza kwa mateso kwa watu wa njia ile baada ya kifo cha Stefano. Unaelezea sababu za Paulo kuanzisha mateso hayo kwa waumini.

Siku hizo

Hii inahusu siku ambayo Stefano aliuawa,

Waaminio wote walitawanyika

Hii ni inavumisha wengi au zaidi ya waamini wa Yerusalem waliyakimbia mateso.

Isipokuwa mitume

Inadhihirisha kwamba mitume walibaki Yerusalem ingawa hawakuyazoea hayo mateso makubwa

Watu wacha Mungu

"Watu wenye hofu ya Mungu" au "Watu waliomuogopa Mungu

Wakafanya maombolezo makubwa

"Wakalia sana ...juu yake"

Aliwaburuza wanaume na wanawake

Sauli aliwachukua kwa nguvu Wayahudi waamini na kuwatoa nje ya nyumba zao na kuwatupa gerezani.

Wanaume na wanawake

inaelezea juu wanaume na wanawake ambao waliokuwa wamemwamini Yesu.

Acts 8:4

Sentensi unganishi

Hapa panaanzia simlizi inayomhusu Filipi, ambaye watu walikuwa wamemchagua kuwa shemasi,

Ambao walikuwa wametawanyika

" waumini ambao walikuwa wametanyika kwa mateso makubwa".

Alienda mpaka Mji wa Samaria

"Kwenda chini" Neno limetumika hapa kwasababu Samaria iko kwenye ukanda wa chini zaidi ya Yerusalemu.

Mji wa Samaria

Haiko wazi kama ni mji wa Samaria katika mji wa Samaria.

akamtangaza Kristo huko

Cheyo "Kristo" kinamwelezea Yesu, Masihi.

Acts 8:6

Wakati makutano ya watu

"Wakati makutano ya watu kutoka mji wa Samaria." Lilikuwa eneo lililobainishwa huko nyuma

Wakaweka umakini

Sababu ya watu kuweka umakini ilikuwa ni uponyaji wote alioufanya Filipo.

Kutoka hapo watu wengi waliosikia, pepo wachafu waliwatoka watu huku wakilia kwa sauti kubwa

"roho wachafu walikuwa wakipaza sauti na kutoka kwa watu waliokuwa nayo.

Na kulikuwa na furaha kubwa katika mji.

Watu wa mji walikuwa na furaha kubwa

Acts 8:9

Maelezo ya jumla

Simoni ametajwa kwenye simlizi hii ya Filipo. Mistari ya 9-11ni maelezo yanayomhusu Simoni ya kuwa alikuwa nani miongoni mwa wasamaria.

Lakini palikuwana mtu mmoja ...jina lake Simoni

Hii ni njia ya kumtambulisha mtu mgeni katika simulizi. Lugha yako pengine inaweza kutumia maneno tofauti kumtambulisha mtu mgeni katika simulizi.

Mji

"Mji wa Samaria"

Wasamaria wote tangu mdogo hata mkubwa

Hii inaongeza chumvi. "Wasamaria wengi katika mji wa Samaria.:

Huyu mtu ni ile nguvu ya Mungu ambayo ni Kuu.

Watu walikuwa wanasema kwamba Simoni ni nguvu ya Mungu inayojulikana Nguvu Kuu.

Acts 8:12

Sentensi unganishi

Mistari hii anatoa maelezo zaidi kuhusu Simoni na baadhi ya Wasamaria waliokuwa wakimwamini Yesu.

Wakabatizwa.

Filipo aliwabatiza waamini wapya

Na Simoni mwenyewe aliamini

Neno "mwenyewe" linatumika kumwelezea Simoni naye aliamini.

Naye alibatizwa

Filipo alimbatiza Simoni pia.

Wakati alipoona ishara na miujiza iliyokuwa ikitendeka, alishangaa

Simoni alishangaa pale alipoona Filipo anafanya ishara na miujiza mikubwa

Acts 8:14

Sentensi unganishi

Luka anaendeleza habari ya kile kilichokuwa kinatokea huko Samaria.

Wakati mitume wa Yerusalemu waliposikia

Alama hii ni ya mwanzo wa sehemu mpya ya simlizi ya waumini walivyokuwa wakiendelea huko Samaria.

Samaria

"Samaria" Neno linaloelezea juu ya watu wengi waliokuwa waumini katika wilaya yote ya Samaria.

Pale waliposhuka chini

"Pale Petro na Yohana waliposhuka chini" kwenda Samaria.

Waliomba kwa ajili yao

"Petro na Yohana waliwaombea waamini wa Samaria"

Kwamba wangepokea Roho Mtakatifu.

"Kwamba Wasamaria wanaoamini wangeweza kupokea Roho Mtakatifu"

Walikuwa tu wamebatizwa

"Filipo alikuwa tu amewabatiza katika Jina la Bwana Yesu Wasamria walioamini"

Ndipo Petro na Yohana wakaweka mikono yao kwao

"Kwao" linahusu watu wa Wasamaria ambao waliamini ujumbe wa injili kutoka kwa Filipo".

Acts 8:18

Roho Mtakatifu ametolewa kupitia kuwekewa mikono ya mitume.

"Mitume waliwapa Roho Mtakatifu kwa kuweka mikono yao juu ya watu"

Kila nitakae mwekea mikono apokee Roho Mtakatifu.

"Kwamba wakati ninaweka mikono yangu juu ya watu, wapokee Roho Mtakatifu"

Acts 8:20

Maelezo ya jumla

Viwalilishi vya majina katika habari hii vinamwakilisha Simoni

pesa yako pamoja na wewe ipotelee mbali

Wewe na pesa yako muangamizwe

Karama ya Mungu

"Karama" ni neno linaelezea uwezo wa kutoa Roho Mtakatifu kwa njia ya kuweka mikono juu ya mtu mwingine.

Hauna sehemu katika jambo hili

Neno "huna sehemu" linaonyesha kuwa Simoni huna sehemu ya kushiriki katika kazi hii.

Moyo wako si mnyoofu

"Kufikiri kwako si sahihi"

Kwa namna ulivyotamani

"Kutaka kununua uwezo wa kutoa nguvu ya roho kwa wengine"

Uovu huu

"Mawazo haya maovu"

labda utasamehewe

"Anaweza kuwa tayari kukusamehe"

Sumu ya uchungu

Haya ni maelezo ya fumbo yanayomaanisha wivu uliokidhiri.

Vifungo vya dhambi

"mtumwa wa dhambi" au "atafanya dhambi tu"

Acts 8:24

Mambo yote mliozungumza yaweza kunitokea

Ujumbe unaweza kuzungumzwa kwa namna nyingine; "Mambo mliyoyazungumza yasiweze kutokea kwangu"

Mambo yote mliozungumza yaweza kunitokea

Ni kemeo la Petro juu ya Simeoni kuadhibiwa kwake na pesa yake pia.

Acts 8:25

Sentensi unganishi

Hapa ni hitimisho la simulizi kuhusu Simoni na wasamaria.

Ushuhuda wa kuzaliwa

Petro na Yohana waliwaeleza wasamaria juu ya wao walivyomfahamu Yesu.

Kunena maneno ya Bwana

Petro na Yohana walielezea juu ya maandiko ambayo Yesu alizungumza kwa wasamaria.

Katika vijiji vingi vya wasamaria

Kwa watu wengi katika vijiji vya Samaria.

Acts 8:26

Sentensi unganishi

Huu ni mwanzo wa simulizi kuhusu Filipo na mwanaume kutoka Ethiopia.

Maelezo ya jumla

Mstari wa 27 unaonyesha taarifa za mwanaume kutoka Ethiopia.

njia iendayo chini ya Yerusalemu kuelekea Gaza

"Iendayo chini" hapa linatumika kwasababu Yerusalemu iko juu zaidi ya Gaza

Sasa

Neno "sasa" ni neno la kiunganishi cha simulizi.

Njia hii iko katika jangwa

Wasomi wengi wanaamini Luka aliongeza mkazo wa kuelezea eneo ambalo Filipo angeweza kupitia.

Tazama

Neno "tazama" linatutahadharisha kwa mtu mpya katika simulizi. Lugha yako inaweza ikawa njia ya kufanya hivi. Kingereza linatumia "Palikuwa na mtu ambaye alikuwa."

Towashi

Mkazo"towashi" hii ni kwamba, Mwethiopia aliyekuwa katika ofisi za serikali kuu.

Kandake

Hiki ni cheo kwa malkia wa Ethiopia . Ni sawa na jinsi "farao" alitumika kuwa mfalme wa Misri.

Kumsoma nabii Isaya

Hili ni agano la kale la Isaya.

Acts 8:29

Sogea karibu na gari hili

Filipo alifahamu kuwa ni muhimu kuwa karibu na mtu yule aliyepanda kwenye mkokoteni.

akamsikia akisoma katika chuo cha nabii Isaya

Hiki ni kitabu cha Agano la Kale cha Nabii Isaya.

Je unafahamu unachosoma?"

Mwethiopia alikuwa mtu mwenye akili na aliweza kusoma, lakini alikuwa na upungufu wa ufahamu wa kiroho. Filipo alimwulija, "Je! Unafahamu maana ya habari unayoisoma?

Nitawezaje, isipokuwa mtu aniongoze kuielewa?"

Swali hili liliulizwa kusisitiza kuwa hakuweza kuelewa bila msaada. ''siwezi mpaka mtu aniongoze"

Alimuomba filipo akae nae

Filipo alikubali kutembea naye akiwa chini ya barabara pamoja naye akiyafafanua maandiko.

Acts 8:32

Maelezo ya jumla

Hiki ni kifungu kutoka katika kitabu cha Isaya

Kama kondoo mbele ya mchungaji akiwa kimya

Mkata manyoya ni mtu ambaye anakata manyoya ya sufu za kondoo ili zitumike.

Kwa kuhuzunishwa kwake hukumu yake iliondolewa

Alidharauliwa na kuhukumiwa bila haki.

Nani ataeleza kizazi chake?

Swali hili lilitumika kuelezea kuwa hatakuwa na uzao. Kwamba; "Hakuna hata mmoja atakayeweza kuzungumzia habari za uzao wake"

maisha yake yameondolewa katika nchi."

Hii inaelezea kifo chake. "Watu walimwua" au "Watu waliyaondoa maisha yake hapa duniani"

Acts 8:34

Nakuomba

"Tafadhari niambie"

ni kuhusu yeye, au za mtu mwingine"

"Je, Ni nabii anazungumzia habari zake mwenyewe, au anamzungumzia mtu mwingine"

katika Isaya

Inamaanisha maandiko ya Nabii Isaya.

Kumhubiria kuhusu Yesu

"kufundisha habari njema kuhusu Yesu kwa matoashi'

Acts 8:36

Wakati wakiwa njiani

Waliendelea na safari njiani

wakafika penye maji

Haiko wazi kama haya "Maji" yalikuwa ya kijito au bwawa la maji au maji mengi. tunachofahamu yalikuwa na kina cha kutosha kuwaza kwenda chini yake.

"Tazama, pana maji hapa nini kinazuia nisibatizwe?,

Towashi alitumia swali hili kumwomba Filipo amruhusu kubatizwa. "Tafadhali niruhusu nibatizwe"

akaamuru gari lisimame.

Akamwambia dereva wa mkokoteni asimame.

Acts 8:39

Sentensi unganishi

Huu ni mwisho wa simulizi kuhusu Filipo na mtu kutoka Ethiopia.

Toashi hakumwona tena

Filipo alitoweka machoni pa Towashi hivyo hakumwona tena.

Filipo akatokea Azoto.

Kulikuwa hamna dalili za Filipo kusafiri kati ya alipokutana na Ethiopia na Azoto. Ghafla alipotelea katika barabara ya Gaza na kuzuka tena Azoto.

Mpaka alipokuja Kaisaria.

Simulizi ya Filipo inaishia Kaisaria.

Acts 9

Matendo 09 Maelezo kwa jumla

Dhana maalum katika sura hii

"Njia"

Hakuna anayefahamu aliyeanza kuwaita Waumini wafuasi wa Njia. Labda Waumini walijiita hivyo kwa vile Bibilia kwa mara nyingi humzungumzia mtu anayeishi maishi yake kama mtu atambeaye njiani. Kama huu ni ukweli, Waumini walikuwa "Wakifuata njia ya Bwana" kwa kuishi kwa njia inayompendeza Mungu.

"Barua kwa Masinagogi ya Dameski"

Kuna uwezekano "Barua" alizoomba Paulo zilikuwa nyaraka za Kisheria zilizoruhusu kuwafunga gerezani. Viongozi wa masinagogi wa Dameski waliiheshimu hiyo barua kwa vile iliandikwa na kuhani mkuu.Iwapo Warumi wangekuwa wameiona hiyo barua, wangemruhusu pia Saulo kuwatesa Wakristo kwa vile waliwaruhusu Wayahudi kuwafanyia watakavyo wale walovunja sheria zao za kidini.

Matatizo mengine ya tafsiri katika sura hii

Alichoona Saulo alipokutana na Yesu

Ni wazi kwamba Saulo aliuona mwanga na kwamba hii ni kwa sababu ya huu mwanga "alianguka chini" Watu wengine hufikiri kwamba Saulo alifahamu ni Bwana alikuwa akimzungumzia bila kuona kiwili cha binadamu kwa vile Biblia huzungumzia kila mara Mungu kama mwanga na kwamba huishi ndani ya Mwanga. Watu wengine hufikiri kwamba baadaye katika maisha yake aliweza kusema,"Nimemuona Bwana Yesu" kwa vile ni umbo la binadamu aliona hapo.

<< | >>

Acts 9:1

Sentensi unganishi

Simulizi inarudi nyuma kwa Sauli na wokovu wake.

Maelezo ya jumla

Mistari hii inatupatia picha kwa kutujulisha kuwa Sauli alikuwa akiendelea na kazi zake tangu Stefano alipouawa kwa kupondwa kwa mawe.

kuendelea kuongea maneno ya mauaji dhidi ya wanafunzi

Kiwakilishi cha jina "mauaji" linaweza tafsiriwa kama kitendo: aliendelea kuongelea vitisho, hata kwa kuwaua wanafunzi.

kwa ajili ya masinagogi

Inazungumzia juu ya watu katika Sinagogi. "Kwa watu wa Sinagogi" au "Kwa viongozi wa Sinagogi"

ili kwamba akimpata

Kama akimpate mtu yeyote

aliye katika Njia ile

"anayeyafuata mafundisho ya Yesu"

Anaweza akawapeleka Yerusalemu

Anaweza akawapeleka kama wafungwa.' "ili viongozi wa wayahudi wapate kuwahukumu na kuwasulubisha".

Acts 9:3

Sentensi unganishi

Baada ya Kuhani Mkuu kumpatia Sauli barua, Sauli alisafiri kuelekea Dameski.

Hata alipokuwa akisafiri

Sauli aliondoka Yerusalemu na kuelekea Dameski.

Ilitokea kwamba

Haya ni maelezo yanayobadisha simulizi kuonyesha kwamba jambo la tofauti litatokea.

ikaangaza kotekote nuru kutoka mbinguni

"nuru kutoka mbinguni ikawangaza kotekote"

Kutoka mbinguni

Inaweza kuwa na maana kuwa; 1) Mbinguni, mahali Mungu anaishi au 2) Anga.

Akaanguka chini

Inawezekana kwamba 1)"Sauli alianguka pekee yake chini"au 2)"Mwanga ulisababisha yeye kuanguka chini"au 3)Sauli alianguka chini kama yeyote ambaye huanguka,"Sauli hakuanguka kwa bahati mbaya.

Kwa nini unaniudhi ?

Bwana alimkemea Sauli katika hali ya swali. "Unaniudhi mimi!"

Acts 9:5

Maelezo ya jumla

Kila kuwakilishi cha neno "wewe" linamaanisha umoja.

Wewe u nani, Bwana

Sauli hakupata kumjua Yesu kama Bwana. Hii ilikuwa ni tatizo kwamba alikuwa kwenye nguvu za ajabu

Lakini inuka ,ingia mjini

"inuka na uende katika mji wa Dameski"

utaambiwa yakupasayo

Mtu mmoja atakuambia

wakisikiliza sauti, wasione mtu

Waliisikia sauti, lakini hawakumwona mtu yeyote.

Bila kumuona yeyote

"Lakini hakumwona yeyote" Bali Sauli aliona mwanga tu.

Acts 9:8

alipofungua macho

Hii inamaanisha Sauli aliyafunga macho kwasababu ya mwanga ulikuwa mkali.

Hata asionne chochote

Sauli alikuwa kipofu.

hakuweza kuona kitu

"Alikuwa kipofu" au "hakuweza kuona chochote"

Hakuweza kula wala kunywa

"hakuweza kula wala kunywa hakuwa na njaa"

Acts 9:10

Maelezo ya jumla

Simulizi inabadilika na kuanza kumtaja mtu aliyeitwa Anania ambae anatambulishwa kwenye simulizi. Huyu sio Anania yule aliyetajwa katika matendo ya mitume 5:1, 3.

Basi palikuwa

Hii inatambulisha wahusika wapya, Anania

Naye alisema

Anania alisema

Inuka uenda zako katika mtaa uitwao Nyofu

Nenda kwenye barabara inayoitwa nyoofu.

Katika nyumba ya Yuda

Yuda si yule mwanafunzi aliyemsaliti Yesu. Yuda alikuwa ndio mmiliki wa nyumba uko Dameski ambapo Anania alikuwa akiishi.

Mtu wa Tarso aitwaye Sauli

"Mtu kutoka katika mji wa Tarso"

kumwekea mikono juu yake

Hii ilikuwa alama ya kumpatia Sauli baraka za kiroho.

Kwamba apate kuona

"Aweze kuona kwa mara nyingine tena"

Acts 9:13

Watu wako watakatifu

Neno "Watu watakatifu" linamaana ya Wakristo. "Watu wa Yerusalemu waliokwisha kumwamini Yesu"

ana mamlaka kutoka kwa kuhani mkuu kumkamata kila mmoja

Inamaana Sauli amepewa nguvu na mamlaka na Kuhani Mkuu, lakini yalikuwa na mipaka kwani ilikuwa ni kwa Wayahudi tu.

Yeye ni chombo teule kwangu

"chombo teule" ni hali ya kutengwa maalumu kwa ajuli ya huduma. "Nimemchagua yeye ili anitumikie.

Kubeba jina langu

Hii ni hali ya kumuelezea na kuongelea kuhusu Yesu. ili anipeleke mimi kwa watu.

Kwa ajili ya jina langu

Hii ni hali ya kuwaelezea watu kuhusu mimi (Yesu).

Acts 9:17

Sentensi unganishi

Anania anaenda katika nyumba ambapo Sauli anaishi. Baada ya kuponywa , simulizi inabadilika kutoka kwa Anania kwenda kwa Sauli.

Anania akaenda, akaingia mle nyumbani;

Anania likwenda kwenye na baada ya kuipata ile nyumba mahali alipokuwepo Sauli akaingia ndani.

Kumwekea mikono

Anania aliweka mikono yake juu ya Sauli

amenituma ili upate kuona na kujazwa roho mtakatifu

"Amenituma ili upate kuona tena na Roho Mtakatifu akujaze"

Kitu kama magamba

"Kitu kilitokea kama magamba ya samaki na kuanguka toka machoni"

akapata kuona

Alikuwa na uwezo wa kuona tena

Aliinuka na akabatizwa

"Sauli aliiuka na Anania akambatiza"

Acts 9:20

Wakati huo huo akamtangaza Yesu

ukumu la kumtangaza Yesu, punde alianza kulifanya.

Akisema kuwa Yeye ni mwana wa Mungu

"Yeye" inaashiria kuwa ni Yesu. Sauli, Baada ya kumwamini Yesu na kumjua Yesu kama 'mwana wa Mungu"

Wote waliomsikiliza

Wengi walipata kusikia habari zake.

Sio mtu yule aliyewaharibu wote wa Yerusalemu walioliitia jina hili?

Hii ni kejeli na swali hasi linalomwelezea Paulo kuwa hakika alikuwa mtu ambaye aliwatesa waamini. "Huyo ni mtu ambaye aliwaharibu wote wa Yerusalemu walioliitia jina hili la Yesu!"

Acts 9:23

Wayahudi

Inamaanisha Wayahudi viongozi.

lakini mpango wao ukajulikana na Sauli

"Lakini mtu mmoja akawaambia mpango wao kwa Sauli" au "Lakini Sauli akafahamu mipango yao juu yake"

Wakamvizia mlangoni

Mji huu ulikuwa na ukuta uliouzunguka.Watu waliingia na kutoka katika mji huo kupitia mlango.

Wanafunzi wake

Watu walioamini ujumbe wa Sauli kuhusu Yesu na walifuatilia mafundisho yake

wakamshusha kupitia ukutani, wakamtelemsha chini katika kapu

Kwa kutumia kamba walimshusha Sauli katika kikapu kikubwa kupitia tundu katika ukuta.

Acts 9:26

Lakini wote walikuwa wakimuogopa

"Walikuwa wote" ni kuimba kwa wingi "karibia wote"

Sauli alihubiri kwa ujasiri katika jina la Yesu

Huu ni mfano wa Sauli anahubiri au anafundisha ujumbe wa injili ya Yesu Kristo.

Acts 9:28

Katika jina la Bwana Yesu

Hii ni injili ya mfano wenye ujumbe wa Yesu Kristo.

Mahojiano na wayahudi wa kiyunani

Sauli alijaribu kutafuta sababu za wayahudi wa kiyunani.

Kumleta chini mpaka Kaisaria

Kaisaria iko chini zaidi ya Yerusalemu. Hata hivyo,ilikuwa kawaida kusema kwamba mmoja alipanda juu Yerusalemu.

na wampeleke aende Tarso.

Kaisari ilikuwa bandari, yawezekana walimpeleka Sauli Tarso kwa njia ya meri.

Acts 9:31

Sentensi unganishi

Katika mstari wa 32, habari inabadirika kutoka simlizi ya Sauli na kuanza simlizi mpya juu ya Petro.

Maelezo ya jumla

Mstari wa 32 ni habari inayotupatia taarifa za kukua kwa kanisa.

kanisa lote katika Uyahudi, Galilaya na Samaria

Hapa ni kiwakilishi cha "kanisa" kama umoja likiwakilisha zaidi ya kusanyiko la waumini. Linaelezea waumini wote katika jumuia zote za Israeli.

lilikuwa na amani

ilikaa kwa amani". Linamaanisha kuwa yale mateso yaliyoanza kwa mauaji ya Stefani yalikuwa yamekoma.

Likajengwa

Hapa mwezeshaji wake ni "Mungu" au "Roho Mtakatifu". "Mungu aliwasaidia wakue" au "Roho Mtakatifu aliwajenga na kuwa imara".

Kutembea katika hofu ya Mungu

"waliendelea kumheshimu Bwana'

Katika faraja ya Roho Mtakatifu

"Roho Mtakatifu aliwaimarisha na kuwapa ujasiri"

Pande zote za mkoa

Hii ni fahari kwa Petro kutembelea waumini wengi pande za Yuda, Galilaya, na Samaria.

Alitelemkia

Neno "Alitelemkia" ilieleza kuelekea Lida iliyo upande wa chini kulinganisha na maeneo mengine alikotembelea Petro.

Lida

Lida ni mji ulioko kati ya kilomita 18 kaskazini mashariki mwa Jafa. Huu mji ulikuwa ukiitwa Lod kwenye Agano la Kale,na katika Israeli ya sasa.

Acts 9:33

Akamuona huko mtu mmoja

Petro hakuwa makini kumtafuta mtu aliyepooza lakini ilimtokea. "Hapo Petro akakutana na mtu."

mtu mmoja jina lake Ainea

Hapa anatambulisha Ainea kama mtu mpya katika simlizi.

Ambaye amekuwa kitandani ...amepooza

Hii ni historia ya nyuma kuhusu Ainea

Aliyepooza

hana uwezo wa kutembea, pengine hakuwa na uwezo wa kujisogeza chini ya kiuno

jitandikie kitanda chako

"jitwike godoro lako"

kila mtu aliyekaa Lida Sharon

Hii inaimarisha maana " watu wengi walioishi maeneo ya Lida na Sharoni.

Wakamwona yule mtu.

Inaweza kuwa msaada kuelezea kuwa walimwona mtu akiwa mtu ameponywa. "Walimwona mtu ambaye Petro alikuwa amemponya".

Acts 9:36

Sentensi unganishi

Luka anaendelea na simlizi ya tukio jipya kuhusu Petro.

Maelezo ya jumla

Mistari hii inatupa historia ya mwanamke aliyeitwa Tabitha.

Palikuwa

Hili linamtambulisha sehemu mpya katika simulizi.

Tabitha, ambalo lilitafsiriwa kama "Dorcas."

Tabitha ni jina lake katika lugha ya kiaramaiki,na jina la Dorcas katika lugha ya Kigiriki. Majina yote yalikuwa na maana ya "paa."

alijaa matendo mema

"anafanya mengi mazuri ya kweli"

Ilitokea katika siku hizo

"Ilitokea wakati Petro alipokuwa Lida".

walipomsafisha

Waliusafisha mwili ikiwa ni maandalio ya maziko yake.

walimpandisha chumba cha juu na kumlaza.

Huu ilikuwa ni utaratibu wa muda wa kuuonyesha mwili wakati wa maandalizi ya mazishi.

Acts 9:38

Waliwatuma watu wawili kwake

"Wanafunzi waliwatuma watu wawili kwake"

Katika chumba cha juu

Chumba cha juu mahali mwili wa Dorkas ulikuwa umelazwa.

Wajane wote

Inawezekana kuwa wajane wote wa mji ule walikusanyika pamoja kwani haukuwa mji mkubwa.

Wajane

wanawake ambao waume zao walifariki na walikuwa wanahitaji kusaidiwa.

Wakati akiwa pamoja nao

"wakati akiwa hai pamoja na wanafunzi"

Acts 9:40

Sentensi unganishi

Simlizi ya Tabitha inaishia katika mstari 42, na mstari 43 unatuambia kilichokuwa kinaendelea kwa Petro baada ya simlizi ya Tabitha kumalizika.

Akawatoa wote nje

Kwa shauri hili, Petro aliwafanya kila mmoja kuondoka ili aweze kuwa pekee yake na kuomba kwa ajili ya Thabitha.

akampa mkono wake akamwinua

Petro alimshika mkono wake na kumsaidia kuinuka.

waumini na wajane,

Hata wajane yawezekana walikuwa waumini, lakini hapa wametambulishwa kwa jina la wajane kwasababu Tabitha alikuwa mtu muhimu kwao.

Jambo hili kujulikana Yafa yote

Muujiza wa Petro kumfufua Tabitha kutoka kwenye kifo ukajulikana na watu wote wa Yafa.

Walimwamini Bwana

"waliiamini injili ya Bwana Yesu."

Ikatokea kwamba Petro alikaa

"Ikatokea kuhusu kwamba Petro akakaa huko kwa muda"

Acts 10

Matendo 10 Maelezo kwa Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Chafu(Najisi)

Wayahudi waliamini kwamba waliamini walitembelea ama kula na watu wa mataifa. Hii ni kwa sababu Wafarisayowalikuwa wameunda sheria kinyume nayo kwa vile walitaka watu wasikule chakula ambacho sheria Musa ilisema ni najisi. Sheria ya Musa ilisema kwamba chakula kingine kilikuwa najisi lakini haikusema kwamba watu hawakustahili kutembelea ama kula na watu wa mataifa. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#clean and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lawofmoses)

Ubatizo na Roho Mtakatifu

Roho Mtakatifu aliwakujia waliokuwa wakimsikiza Petero. Hii inaonyesha Waumini Wayahudi kwamba watu wa Mataifa wangepokea neno la Mungu na kupokea Roho Mtakatifu vile waumini Wayahudi walivyopokea. Baada ya hiyo,Watu wa Mataifa walibatizwa.

<< | >>

Acts 10:1

Sentensi unganishi

Huu ni mwanzo wa sehemu juu ya habari inayohusu Kornelio.

Maelezo ya jumla

Mistari hii inatupa mrejesho wa taarifa kuhusu yeye.

Kulikuwa na mtu fulani

Hii ilikuwa ni njia ya kutambulisha mtu mwingine katika habari.

jina lake aliitwa Cornelio, alikuwa mkuu wa kikosi cha Kiitalia

"jina lake aliitwa Kornelio. alikuwa ni mtu mwenye cheo wa maaskari 100 kutoka Italia katika sehemu ya jeshi la Rumi"

Alikuwa mcha Mungu na alimwabudu Mungu

"Aliamini katika Mungu na alitaka kumtii Mungu na kumwabudu Mungu katika maisha yake"

na nyumba yake yote

"na watu wote wengine wa nyumbani kwake ambao pengine walikuwa wa mataifa walimcha Mungu"

aliomba kwa Mungu siku zote.

Alikuwa akimwomba Mungu wakati wote.

Acts 10:3

saa tisa

Hii ni muda wa Alasiri wa kawaida uliokuwa ukitumiwa na wayahudi kwa maombi.

akaona kwa wazi

Kornelio aliona kwa wazi"

Maombi yako na zawadi zako kwa masikini zimepanda juu kama kumbukumbu kwenye uwepo wa Mungu

Inamaanisha kuwa Misaada ya Kornerio kwa wahitaji pamoja na maombi yalimpendeza Mungu na kuwa ukumbusho kwake.

mtengenezaji wa Ngozi

Mtu mtaalamu wa kutengeneza ngozi za wanyama.

Acts 10:7

Baada ya Malaika aliyekuwa akisema naye kuondoka

"Baada ya maono ya Kornelio kufika mwisho"

Askari aliyekuwa akimwabudu Mungu kutoka miongoni mwa maaskari waliokuwa wakimtumikia.

Moja ya maaskari waliokuwa wakimtumikia Kornelio ambao pia walikuwa wakimwabudu Mungu. Ilikuwa mara chache sana jeshi la kirumi, ambapo Kornerio na maaskari wengine kumcha Mungu, alihali wenginge hawamchi Mungu.

aliwaambia yote yaliyotokea

Kornerio alielezea maono yake kwa watumishi wake wawili na kwa mmoja wa maaskari wake.

akawatuma Yafa

"aliwatuma wawili wa watumishi wake na askari mmoja huko Yafa"

Acts 10:9

Sentensi unganishi:

Habari inabadilika kutoka kwa Kornelio kutuambia kile Mungu alikuwa anakifanya kwa Petro.

Wakati wa saa sita

"Ilikuwa saa sita mchana"

juu darini

Mapaa ya nyumba yalikuwa tambarare, na watu mara nyingi walifanya kazi mbalimbali juu yake.

wakati watu wanapika chakula,

"Kabla watu hawajamaliza kutayarisha chakula cha mchana"

Aliona maono

"Mungu alimpa Petro maono" au "Aliona maono"

akaona anga limefuguka

Huu ulikuwa ni mwanzo wa Maono ya Petro.

kitu fulani kama nguo kubwa ikishuka chini kwenye ardhi katika kona zake zote nne

Ndani ya chombo kilikuwa na wanyama na mwonekano wake ni kama nguo kubwa ya pembe nne.

kikishuka chini katika pembe zake nne.

"Kitambaa kikiwa na pembe zake nne juu zaidi ya kingine.

aina zote za wanyama wenye miguu minne na watambaao juu ya ardhi, na ndege wa angani

Wanyama wenye miguu... ndege wa angani. Mwitikio wa Petro kwa maono yale mstari unaofuata unaonyesha Wayahudi walikuwa wamepewa amri ya kutokula baadhi ya hao wanyama. "Wanyana na ndege ambao sheria ya Musa ilizuia wasipate kuliwa"

Acts 10:13

sauti ikasema kwake

Mtu anayeongea hajulikani. Pengine "sauti" alikuwa Mungu mwenyewe, ingawa inawezekana alikuwa Malaika kutoka kwa Mungu.

Siyo hivyo

Petro anaapa "Sitafanya hivyo"

sijawahi kula kitu chochote najisi na kichafu

Imetafsiriwa kuwa wanyama wanawakilisha wasio safi kama ilivyoelezwa na sheria ya Musa na walikuwa hawaliwi na waumini walioishi kabla ya kifo cha Kristo.

Alichokitakasa Mungu

Kama Mungu ndiye msemaji, anajipambanua mwenyewe kwa nafsi ya tatu; "Kile ambacho Mungu alikitakasa"

Hii ilitokea mara tatu

Si kwamba kila kitu alichokiona Petro kilitokea mara tatu. Hii inaweza kuwa na maana; "Kile ambacho Mungu alikitakasa" neno hili ndilo lilijirudia mara tatu mfurulizo.

Acts 10:17

Petro akiwa katika hali ya kuchanganyikiwa

Inamaana kuwa Petro alikuwa na wakati mgumu kuelewa maana ya maono hayo.

Tazama

Neno "Tazama" hapa linatutazamisha sisi kuwa makini katika taarifa za ajabu ambazo zinafuata, kwa jambo hili, wanaume wawili walisimama mbele ya geti.

wakasimama mbele ya geti

"kusimama mbele ya geti la kuingilia ndani." hii inamaanisha kuwa hii nyumba ilikuwa na ukuta na geti la kuingilia kwenye nyumba hiyo.

wakiuliza njia ya kwenda kwenye nyumba

Hili nitukio lilitendeka kabla ya kufika kwenye nyumba alipokuwa Petro. Hili tukio lingeripotiwa mapema kabla.

Na wakaita

Watu wa Karnelio walibaki nje ya Geti wakati wakiulizia kuhusu Petro.

Acts 10:19

akiwaza juu ya hayo maono

"Wakati Petro alipokuwa akifikri juu ya haya maono"

Roho

"Roho Mtakatifu"

Tazama

Uwe macho" au "Amka"

watu watatu wanakutafuta

Baadhi ya nyaraka za kale zinasema idadi tofauti ya wale watu.

Shuka chini

"Shuka chini kutoka dari ya nyumba"

Usiogope kwenda nao

Ingekuwa kawaida kwa Petro kutokwena na hao watu; 1) Kwa vile walikuwa wageni kwake na 2) Walikuwa wa mataifa ambapo Wayahudi walikuwa hawachangamani na wao.

Mimi ni yule mnayemtafuta

"Mimi ndiye mtu yule mnayemtafuta"

Acts 10:22

Wakasema

"Wale wajumbe watatu kutoka kwa Kornelio wakasema kwa Petro"

hupenda kumwabudu Mungu

Neno "Kumwabudu" Lina maana ya nia ya ndani kuheshimu na kicho cha kweli.

taifa lote la kiyahudi

Hii ni mfano kwa ajili ya tabia nzuri ya Kornelio ilikuwa inajulikana vizuri kwa watu wengi wa Kiyahudi.

Petro akawakaribisha kuingia ndani na kukaa pamoja naye

Safari ya kuelekea Kaisaria ilikuwa ndefu sana kwa wao kuanza muda wa mchana.

kukaa pamoja naye

"Wajumbe wa Kornerio wakawa wageni wake"

ndugu wachache kutoka Yafa

Hii inaelezea juu ya waumini waliokuwa wakiishi Yafa.

Acts 10:24

Siku iliyofuata

Hii ilikuwa ni siku moja baada ya wao kuondoka Yafa. Safari ya kwenda Kaisaria ilikuwa ndefu zaidi ya siku moja.

Kornelio alikuwa akiwasubiri

Kornerio alikuwa akiwatarajia. Akiwa amewaita pamoja ndugu zake na marafiki zake wa karibu

Acts 10:25

Wakati Petro akiingia ndani

"Mara Petro alipoingia ndani ya nyumba"

Kornerio akainama hadi chini kwenye miguu yake

Ingawa kuinama lilikuwa ni tendo la kawaida katika utamaduni wao, Kornerio yeye aliinama kwa Petro kama ishara ya kumsujudia.

Simama; mimi mwenyewe pia ni mwanadamu

Hili ni kukemea vikali au marekebisho kwa Kornelio kuwa asimwabudu Petro.

Acts 10:27

Sentensi unganishi:

Petro anawaelekea watu waliokuwa wamekusanyika kwenye nyumba ya Kornelio.

watu wengi wamekusanyika pamoja

"akakuta wamataifa wengi wamekusanyika pamoja." hii inamaanisha kuwa watu ambao Kornelio alikuwa amewaalika walikuwa wamataifa.

Ninyi wenyewe mnajua

Petro anamlenga Korneria na wageni aliokuwa amewaalika.

siyo sheria ya kiyahudi

"imefichika kwa wayahudi"

mtu ambaye si wa taifa hili.

Anaelezea watu ambao hawakuwa wayahudi, bila kutaja maeneo maalumu walikokuwa wanaishi.

Acts 10:30

Sentensi unganishi:

Kornelio akajibu swali la Petro.

Maelezo ya jumla:

Mstari wa 31na 32 Kornelio ananukuu kile malaika alisema alipojitokeza kwake wakati wa saa tisa.

Siku nne zilizopita

Kornerio anafafanua juu ya siku kabla ya usiku wa siku kabla ile kabla hajaongea na Petro. Utamaduni wa Kibiblia unahesabu siku hiyo. Hivyo kabla ya siku tatu zilizopitz za usiku ilihesabiwa kuwa "siku ya nne iliyopita." Mila za Magharibi ya sasa, hii inawezakuwa, "Siku tatu zilizopita."

Wakati nikiomba

maandiko ya kale yanasema "kufunga na kuomba" badala ya kuomba tu"

muda wa saa tisa

Mchana wa kawaida ni wakati wa Wayahudi kuomba kwa Mungu.

maombi yako yamesikiwa na Mungu

Inamaanisha Mungu amesikia maombi yako

ukumbusho mbele za Mungu

"Mungu amekuletea ukumbusho" Hii haimanishi kuwa Mungu alikuwa amesahau.

akamwite mtu mmoja anayeitwa Simoni aje kwako

"Mwambie Simoni anayeitwa Petro kuja kwako"

Umetenda wema kuja

Hii ni namna ya heshima ya kumshukuru Petro kwa kuja kwake.

katika macho ya Mungu

Hii inadhihirisha uwepo wa Mungu.

Acts 10:34

Sentensi unganishi

Petro anaanza hotuba kuongea na kila mtu ndani ya nyumba ya Kornelio.

Ndipo Petro akafungua mdomo wake na kusema

"Petro alianza kuzungumza kwao"

Hakika

Hii inamaanisha kile anachokwenda kukisema kina umuhimu wa kukijua

Mungu hawezi kuwa na upendeleo

"Mungu hapendelei watu maalumu"

kila mtu yeyote anayemwabudu na kufanya matendo ya haki anakubalika kwake

"anamkubali kila mtu anayemwabudu na kufanya matendo ya haki"

Ibada

Neno "Ibada" linamaanisha nia ya ndani ya heshima na kicho cha kweli.

Acts 10:36

Sentensi unganishi

Petro anaendelea na Kornerio pamoja na wageni wake.

ambaye ni Bwana wa wote

"Wote" maana yake watu wote"

Yudea yote

"Katika maeneo mbalimbali ya Yudea"

baada ya ubatizo ambao Yohana alitangaza

"Baada ya Yohana kuhubiri kwa watu kurubu na kubatizwa"

Mungu alivyomtia mafuta kwa Roho Mtakatifu na kwa nguvu

Roho Mtakatifu na nguvu za Mungu zimenenwa kana kwamba ni vitu vinaweza kumiminwa juu ya mtu.

wote walioteswa na ibilsi

"Watu wengi waliokuwa wanapitia mateso ya shetani"

Mungu alikuwa pamoja naye.

Inamaanisha; "Mungu alikuwa akimtia nguvu kuzitenda kazi zote"

Acts 10:39

Maelezo ya jumla

Petro na Mitume na waumini ambao walikuwa pamoja na Yesu wakati akiwa hapa duniani.

Katika nchi za Wayahudi

Inaelezea zaidi Yudea ya wakati huo.

ambaye waliyemuua

"ambaye viongozi wa kiyahudi walimwua''

Wakamtundika juu ya mti

Inamaanisha, "kumuwamba Yesu katika mti wa msalaba"

Huyu mtu

"Huyu mtu Yesu"

Mungu alimfufua

"Mungu alimfanya kuishi tena"

siku ya tatu

"Siku ya tatu baada ya kufa kwake"

kumpa kujulikana

"alimpa kujulikana na wengi"

kutoka kwa wafu

"Kutoka miongoni mwa waliokwisha kufa" Linafafanua juu ya roho za watu waliokwisha kufa. Kurejea kutoka miongoni mwa hizo roho ni kuwa mzima tena.

Acts 10:42

Sentensi unganishi

Petro anamalizia hotuba yake katika nyumba ya Kornerio aliyokuwa ameianza.

kuwa huyu ndiye ambaye Mungu alimchagua

Mungu alikuwa amemchagua Yesu Kristo.

walio hai na waliokufa

Anamaanisha, " Watu walio hai na watu waliokwisha kufa

Katika yeye manabii wote washuhudie

"Manabii wote walishuhudia habari za Yesu".

kila anayeamini katika yeye atapokea msamaha wa dhambi

Mungu atasamehe dhambi za kila mmoja anayemwamini Yesu kwasababu ya kile Yesu ametenda.

kupitia jina lake

Neno "jina" Linaelezea matendo ya Yesu. Jina lake linamaanisha Mungu huokoa.

Acts 10:44

Roho Mtakatifu akawajaza wote

Neno "Kuwajaza" maana yake ni kutokea ghafla. "Roho Mtakatifu ghafla alishuka".

wote waliokuwa wakisikiliza

Neno "wote" linaelezea kuwa; "Wamataifa ndani ya nyumba waliokuwa wakimsikiliza Petro".

Watu wale wanaohusika na kikundi cha waamini waliotahiriwa

Hii ni namna nyingine ya kuzungumzia juu ya Waumini Wayahudi

Karama ya Roho Mtakatifu

Inaelezea juu ya Roho Mtakatifu mwenyewe aliyetolewa kwao.

Roho Mtakatifu aliyemwagwa

Mungu alimtoa Roho Mtakatifu. "Zawadi ya bure"

Pia na kwa mataifa

Neno "pia" linaonyesha ukweli kuwa Roho Mtakatifu alikuwa tayari ametolewa kwa Wayahudi waumini

Acts 10:46

Sentensi unganishi

Huu ni mwisho wa sehemu ya simlizi kuhusu Kornerio.

wamataifa wanaongea kwa lugha zingine na kumwabudu Mungu

Zilijulikana kuwa ni lugha zilizokuwa zinatamkwa na waliojazwa na Roho Mtakatifu, kilichofanya Wayahudi kukubali kwamba wamataifa nao walikuwa wakimtukuza Mungu.

Kuna mtu yeyote anaweza kuzuia maji ili watu wasibatizwe, Watu hawa wamempokea Roho Mtakatifu kama sisi?

Petro alilitumia swali hili kuwashawishi Wayahudi wakristo kwamba Wamataifa walioamini wanaweza kubatizwa.

Ndipo akawaamuru wabatizwe

Inamaanisha kwamba Wayahudi wakristo ndio waliowabatiza Wamataifa siku hiyo.

wabatizwe kwa jina la Yesu Kristo

"Kwa Jina la Yesu Kristo" Linaelezea kuwa sababu ya kubatizwa kwao ni kwa kumwamini Yesu Kristo.

Acts 11

Matendo 11 Maelezo kwa Ujumla

Dhana Maalum katika sura hii

"Watu wa mataifa pia walipokea neno la Mungu"

Karibu waumini wote wa kwanza walikuwa Wayahudi. Luka anaandika katika sura hii kwamba watu wengi wa mataifa walianza kumwamini Yesu. Waliamini kwamba habari ya Yesu ilikuwa habari ya kweli, vile wakaanza "kulippokea neno la Yesu." Baadhi ya waumini katika Yerusalemu hawakuamini kwamba watu wa Mataifa pia wangekuwa wafuasi halisi wa Yesu. Kwa hivyo Petero alienda akawaambia kilichokuwa kimemtendekea na jinsi alivyowaona watu wa mataifa wakilipokea neno la mungu na kupokea Roho Mtakatifu.

<< | >>

Acts 11:1

Sentensi unganishi

Petro anaingia Yerusalemu na anaanza kuongea na Wayahudi wa huko.

Maelezo ya jumla

Huu ni mwanzo wa tukio jipya katika simlizi

Sasa

Linaashiria sehemu mpya ya simlizi

Ndugu

"Ndugu" Linamaanisha waumini katika Yudea.

waliokuwa Yudea

"Waliokuwa wakiishi mkoa wa Yudea"

Walikuwa wamelipokea neno la Mungu

Linamaanisha kuwa Wamataifa walikuwa wameupokea ujumbe wa Injili kuhusu Yesu. "Waliamini ujumbe wa Mungu kuhusu Yesu Kristo".

Walikuwa wamepanda kwenda Yerusalemu

Yerusalemu ilikuwa juu zaidi ya kila eneo la Israeli. hivyo ilikuwa kawaida kwa Waisraeli kusema wanapanda juu kwenda Yerusalemu.

lile kundi la watu waliotahiriwa

Wayahudi walioamini kwamba kila anayeamini lazina atahiriwe.

watu wasiotahiriwa

Linamaanisha, "watu wa Mataifa"

Alikula pamoja nao

Ilikuwa kinyume kwa utamaduni wa Wayahudi, Wauahudi kula na Wamataifa.

Acts 11:4

Sentensi unganishi

Petro anawajibu Wayahudi kwa kuwaambia juu ya maono na kile kilichotokea katika nyumba ya Kornerio.

Petro alianza kueleza

Petro hakujaribu kusema maneno ya kuwapinga Wayahudi waumini, bali alijibu kwa maelezo ya kirafiki na hekima.

Kwa undani

"Hakika ya kile kilichotokea"

Kama kitambaa kikubwa

Chombo kilichoshikilia wanyama kilionekana kitambaa kikubwa.

Chenye pembe nne

"Kikubwa chenye pembe nne"

wanyama wenye miguu minne waishio katika nchi,

"Wanyama wa miguu" Mwitikio wa Petro ulilenga sheria ya Musa iliyokuwa inazuia kula baadhi ya wanyama.

Wanyama wa mwitu

Pengine ni wanyama wasioweza kufugwa.

wanyama watambaao

Hawa ni wale waendao kwa kutambaa.

Acts 11:7

nikasikia sauti

Sauti ilinena lakini bila yeyote kujidhihirisha. "Sauti" yawezekana ni Mungu, ingawa inawezekana kuwa ilikuwa sauti ya Malaika.

Siyo hivyo

"Siwezi kufanya hivyo" linganisha na sura 10:13.

mdomoni mwangu hakujawahi kuingia kitu chochote kisicho kitakatifu

Wanyama waliokuwa kwenye kitambaa walikuwa ni wanyama ambao sheria ya Wayahudi katika Agano la Kale iliwazuia wasiweze kuwala.

Kichafu

Katika Agano la Kale Sheria ya Wayahudi, mtu alionekana mchafu katika njia mbalimbali, kama vile kula wanyama waliokuwa hawaruhusiwi kuliwa.

kile Mungu alichokitangaza kuwa ni safi, usikiite najisi

Sentensi hii inaelezea juu ya wanyama waliokuwa kwenye kitambaa kikubwa cha pembe nne.

Hii ilitokea mara tatu

Si kila tukio lilirudiwa kuonekana mara tatu, Hata hivyo neno; "Kile Mungu alichokitakasa usikiite najisi" Ni neno lilijirudia mara tatu kwa Petro. Linganisha na sura 10:13.

Acts 11:11

Tazama

Hili neno linaashiria kuanza kutajwa watu wengine kwenye simlizi hii.

Mara moja

"Mara hiyo bila kuchelewa"

Walikuwa wametumwa

"Mtu fulani alikuwa amewatuma"

na nisitofautiane nao.

"Kwamba nisipate cha kunitofautisha nao kwamba walikuwa wamataifa"

Hawa wanaume sita wakaenda pamoja na mimi

anaume sita wakaenda nami mpaka Kaisaria.

Hawa ndugu sita

"Hawa sita Wayahudi waumini"

Ndani ya nyumba ya mtu mmoja

Linaelezea nyumba ya Kornerio

Simoni aliyeitwa Petro

"Simoni ambaye pia aliitwa Petro"

utaokoka

Inaweza kuwa "Mungu atakuokoa"

Na wote wa nyumba yako

Linamaanisha; Wote wataokolewa walioko nyumbani mwako"

Acts 11:15

Maelezo ya jumla

Hapa Petro anajumuisha yeye, Mitume na Wayahudi waumini wote waliopokea Roho Mtakatifu katika siku ya Pentekoste.

Nilipoanza kusema nao, Roho mtakatifu akaja juu yao

namaanisha kwamba, "Petro kabla hajamaliza kunena, kwa vile alikuwa amenuia kusema nao zaidi, Roho Mtakatifu akaingilia kati kwa kuwashukia.

Roho mtakatifu akaja juu yao kama alivyokuja kwetu mwanzoni.

Roho Mtakatifu alishuka kwa wamataifa walioamini kama vile alivyofanya kwetu siku ya Pentekoste.

mtabatizwa katika Roho mtakatifu

Mungu atawabatizeni ninyi katika Roho Mtakatifu.

Acts 11:17

Sentensi unganishi

Petro anamalizia hotuba yake aliyokuwa ameianza katika sura 11:4 kwa Wayahudi juu ya maono yaliyotokea katika nyumba ya Korinerio.

Pia kama Mungu ametoa zawadi... mimi ni nani, kwamba naweza kumpinga Mungu?

Petro anatumia swali hilikueleza kuwa yeye alikuwa anafanya vile kwa kumtii Mungu.

Zawadi sawa

Petro anaelezea zawadi ya Roho Mtakatifu.

Waliposikia mambo haya, hawakurudisha,

"Walinyamaza, hawakuweza tena kumshambulia Petro.

Mungu ametoa toba kwa ajili ya uzima.

"Ametoa toba kwa wote kuwaongoza katika uzima wa milele"

Acts 11:19

Sentensi unganishi

Luka anaelezea kuhusu kile kilichotokea kwa waumini waliokimbia baada ya kuuawa kwa Stefano kwa mawe.

Sasa

Luka anatambulisha simlizi mpya

waamini ambao mateso yalianzia kwenye kifo cha Stephano walitawanyika kutoka Yerusalemu-waamini hawa walienda mbali,

Mateso yaliyoanza na kifo cha Stefano yalisababisha waumini kukimbia na kusambaa maeneo mbalimbali.

Wayahudi peke yake

Waumini walidhani ujumbe wa Mungu ulikuwa kwa ajili ya Wayahudi pekee na siyo kwa wamataifa pia.

na kusema na wayunani

Watu aliokuwa wakiongea kiyunana nao walikuwa ni watu wa mataifa hawakuwa Wayahudi.

Na mkono wa Bwana ulikuwa pamoja nao

Mkono wa Mungu unamaanisha nguvu zake. "Mungu alikuwa na nguvu kuwawezesha wale waumini kuhubiri kwa ujasiri".

na kumgeukia Bwana

Wengi waliacha kuiamini miungu yao ya zamani, na walimwamini Yesu.

Acts 11:22

Maelezo ya jumla

Katika mistari hii Luka anaanza kumtaja Barnaba na wakati huo huo akiwataja waumini wa kanisa la Yerusalemu.

masikioni mwa kanisa

apa neno "masikio" linamaanisha Waumini walisikia habari za matukio.

kuona karama ya Mungu

"Kuona neema ya Mungu" au "Namna gani Mungu ametenda kwa ukarimu juu ya waumini".

aliwatia moyo wote

"Aliendelea kuwatia moyo"

kubaki na Bwana

"kubaki waaminifu katika Bwana" au"Kuendelea kumtumaini Bwana"

Kwa miyo wao wote

"Kwa utimilifu; au Bila kupungukiwa"

amejazwa na Roho Mtakatifu

Barnaba aliongonzwa na Roho Mtakatifu kwa vile alikuwa amemtii.

watu wengi wakaongezeka katika Bwana

"Kuongezeka" Walioamini walizidi kuongezeka.

Acts 11:25

Maelezo ya jumla

Luka anazungumzia kuhusu Barnaba na Sauli.

Kwenda Tarso

"Alitoka kuelekea Tarso"

kumwona Sauli...Alipompata, akamleta Antiokia

Inaonyesha Barnaba alichukua muda na bidii kumtwaa Sauli kutoka Tarso.

Ikawa

neno linaonyesha mwanzo wa tukio jingime katika simlizi hiyo.

wakakusanyika pamoja na kanisa

"Barnaba na Sauli wakakusanyika pamoja na kanisa."

Na wanafunzi wakaitwa wakristo kwa mara ya kwanza

Inamaanisha kuwa watu wengine walikuwa wakiwaita waumini kwa jina hili. "Watu wa Antiokia waliwaita wanafunzi wakristo"

Kwa mara ya kwanza

"Kwa mara ya kwanza huko Antiokia"

Acts 11:27

Maelezo ya jumla

Luka anaelezea historia kuhusu unabii huko Antiokia.

Sasa

Neno hili linatumika kuweka kituo katika simlizi hiyo kuu.

manabii wakashuka kutoka Yerusalemu mpaka Antiokia

Yerusalemu ilikuwa juu zaidi ya Antiokia, hivyo ilikues kawaida ya Waisraeli kusema wanapanda kwenda Yerusalemu

Agabo ndilo jina lake

"Jina lake alikuwa akiitwa Agabo

akiashiriwa na Roho

"Roho Mtakatifu alimwezesha kutoa unabii"

njaa kali itatokea

"Upungufu mkubwa wa chakula utatokea"

Juu ya dunia yote

Akimaanisha, "Katika dola yote ya Kirumi"

wakati wa siku za Klaudio.

Wasikilizaji wa Luka wangejua kwamba Klaudio alikuwa Mtawala wa Rumi wakati huo.

Acts 11:29

Maelezo ya Jumla

Sura hii wanaotajwa ni waumini wa kanisa huko Antiokia

Kwa hiyo

Neno linaloelezea kuwa jambo lililotokea kwasababu ya kitu kingine pia

kila mmoja alivyo fanikiwa,

atu matajiri walituma misaada zaidi, na wale masikini walituma kwa kiasi chao.

kwa ndugu walioko Uyahudi

"Kwa wakristo waliokuwa huko Yudea"

kwa mkono wa Barnaba na Sauli.

"Chini ya usimamizi wa Barnaba na Sauli"

Acts 12

Matendo 12 Maelezo kwa jumla

Muundo na Mpangilio

Sura ya 12 inatuelezea kilichomtendekea mfalme Herode wakati Barnabas alikuwa anamrudisha Saulo kutoka Tarshishi na wakipeleka pesa kutoka Antiokia kwa watu wa Yerusalemu (11:25-30). Aliwaua viongozi wengi akamfunga Petero gerezani. Baada ya Mungu kumsaidia Petero kutoroka gerezani, Herode aliwaua walinzi wa gereza kisha naye akauwawa na Mungu. Luka anatuelezea katika mstari wa mwisho wa sura hii jinsi Barnaba na Saulo waliyorudi kutoka Antiokia.

Mifani ya usemi muhimu katika hii sura

Kuwa na mfano wa kibinadamu

"Neno la Mungu" linazungumziwa kana kwamba ni kiumbe kinachoweza kumea na kuzaana. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#wordofgod and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-personification)

<< | >>

Acts 12:1

Sentensi unganishi

Hapa tena panaanza mateso upya. tukio la kwanza ni la kuuawa kwa Yakobo na kisha kukamatwa kwa Petro na kutiwa gerezani na baadaye kuwa huru.

Maelezo ya jumla

Hii ni historia kuhusu Herode kumwua Yakobo.

Sasa

Hii inaanzisha mwanzo wa simulizi.

Wakati huo

Neno linalotambulisha wakati au kipindi cha njaa.

akanyosha mkono wake

Inamaanisha Herode alikuwa ameanza kuwakamata waumini.

wale wanaotoka kwenye kusanyiko

Ni Yakobo na Petro pekee wanatajwa kuashiria huwa hawa walikuwa viongozi wa kanisa la Yerusalemu.

ili kuwatesa

"Kusababisha mateso kwa waumini"

Akamwuua Yakobo nduguye Yohana kwa upanga.

Hii inaonyesha namna Yakobo alivyouawa.

Akamwua

Inamaanisha ama "Herode Mfalme alimwua" au "Herode Mfalme aliagiza kuua."

Acts 12:3

Maelezo ya jumla

Neno la kiwakilishi hapa linamaanisha Mfalme Herode.

Baada ya kuona kuwa inawapendeza Wayahudi

erode alitambua kuwa mauaji ya Yakobo yalikuwa yamewafurahisha Wayahudi"

Kuwapendeza Wayahudi

"Wayahudi viongozi walipendezwa na tukio hilo"

Hiyo ilikuwa

"Herode alifanya hivi" au "Hii ilitokea"

Siku za mikate isiyochachwa

Inadokeza sikuku ya dini ya Kiyahudi ya Pasaka. "Ni muda huu Wayahudi walikuwa wakila mkate usiotiwa chachu."

vikosi vinne vya askari

"Vikosi vinne vya askari". Kila kikosi kilikuwa na askari wanne vilivyo mlinda Petro. Kila kikosi kimoja baada ya muda uliogawanywa katika saa ishrini na nne. kila mara askari wawili wangekuwa karibu na Petro alihali askari wawili wakiwa kwenye lango.

alikuwa akitarajia kumpeleka kwa watu

Herode alikuwa amepanga kumhukumu Petro mbele ya macho ya Wayahudi.

Acts 12:5

Petro akawekwa gerezani,

Inamaanisha Maaskari waliendelea kumlinda Petro ndani ya gereza.

lakini maombi yakafanywa kwa bidii na kusanyiko kwa ajili yake

Kundi la waumini wa Yerusalemu kwa nia moja walimwomba Mungu kwa ajili yake.

Kwa nia moja

"Walizidi kujikabidhi" au "Kwa nia moja bila kukatisha maombi"

Herode alikuwa anatarajia kumtoa nje

Herode alikuwa amepanga kumtoa Petro nje ya gereza ili kumhukumu.

amefungwa na minyororo miwili,

"alifungwa kwa minyororo miwili". Kila mnyororo ulikuwa umeunganishwa kwa walinzi wawili walioketi karibu na Petro.

Wakilinda gereza.

"Wakifanya kazi yao ya ulinzi"

Acts 12:7

Tazama

Neno linaloashiria kuzingatia kwa taarifa za kushangaza zilizokuwa zinakwenda kutokea.

Upande wake

"Anayefuata" au "Upande wake"

Ndani chumbani

"ndani ya chumba cha gereza"

Akampiga Petro ubavuni

"Malaika alimpiga ili kumwamsha Petro" Petro alikuwa na usingizi mzito kiasi kwamba ilikuwa inahitajika kuamshwa.

minyororo aliyokuwa amefungwa ikafunguka

Malaika alisababisha minyororo kuanguka kutoka kwa Petro bila ya kuigusa.

Petro akafanya hivyo

Petro alifanya kile aliagizwa kufanya na Malaika. Petro alitii.

Acts 12:9

Hakujua

"Hakuwa anajua kilichokuwa kinaendelea"

kilichofanywa na malaika kama ni cha kweli

Tukio la Malaika kwa Petro lilikuwa la kweli.

Baada ya kupita lindo la kwanza na la pili

Askari hawakuwa na uwezo wa kumwona Petro na malaika wakitembea mpaka kutoka lango la nje.

walipita

"Waliweza kupita"

Lindo la pili

"Katika lindo la pili nako wakapita"

Wakafika

"Walilifikia lango kuu"

Lililoelekea mjini

"Lilifunguka kutoka gerezani kuelekea mjini"

likafunguka lenyewe

Si Petro wala Malaika aliyelifungua lango hilo.

wakashuka kwenye mtaa,

"Wakatembea wakiwa barabarani"

Malaika akamwacha.

"Mara Malaika akamwacha" au "Ghafla akatoweka"

Acts 12:11

Petro alipojitambua

"Petro alipopata ufahamu alitambua kuwa tukio lilikuwa halisi"

ili kunitoa katika mikono ya Herode,

ungu ameniokoa na mkono mbaya wa Herode uliopangwa kwa ajili yangu"

na kwa matarajio ya watu wote wa uyahudi

"Kwamba Wayahudi viongozi walidhani ingefanikiwa kwa Petro kuuawa"

Baada ya kujua haya

Herode alitambua kuwa Mungu alikuwa amemwpusha Petro na hukumu ya yake.

Yohana ambaye ni Marko

"Yohana ambaye pia aliitwa Marko"

Acts 12:13

Maelezo ya jumla

Maelezo haya yanawataja binti Rhoda pamoja na wote waliokuwa wakiomba mle chumbani.

Alibisha mlangoni

"Petro alibisha mlangoni" Alizidi kugongagonga kama ilivyokuwa desturi ya Wayahudi ili kuruhusu waliopo kujua kuwa wametembelewa.

kwenye mlango wa kizuizi

"Katika mlango wa nje" au "Katika mlango wa kuingilia kutoka barabarani hadi kwenye yadi ya nyumba"

Akaja kufungua

"Alikuja getini kuuliza ni nani aliyekuwa anabisha hodi"

Kwa furaha

"Kwa vile alijawa na furaha" au "Furaha kupita kiasi"

Alishindwa kuufungua mlango

"Hakuweza kuufungua mlango" au "Alisahau kufungua mlango"

akakimbia ndani ya chumba

"Alikwenda mbio kwenye chumba cha nyumba ile"

na kuwajulisha

liwajulisha au "Alisema"

Petro amesimama mbele ya Mlango

"Amesimama nje mbele ya mlango"

Wewe ni mwendawazimu

Watu siyo tu hawakumwamini, bali walimkemea pia kwa kusema maneno ya kipuuzi.

lakini alikazia kuwa ni kweli

"Alisisitiza kusema alichowaambia kilikuwa cha kweli"

Wakamwambia

"Walimwambia"

Ni malaika wake

"KIle ulichokiona ni malaika wa Petro" Wayahudi waliamini kuwa na malaika mlinzi na inawezekana walifikiri kwa Petro hivyo, kuwa malaika wa Petro alikuwa amekuja kwao.

Acts 12:16

Maelezo ya jumla

Ingawa Herode alikuwa amemwua Yakobo sura 12:1, hata hivyo kulikuwa na Yakobo zaidi ya mmoja.

Lakini Petro aliendelea kubisha

Neno "Kuendelea" linamaanisha Petro alifuluriza kubisha kwa mudo wote wale wa ndani wakiwa wanazungumza habari zake.

Wajulishe haya mambo

"Waambieni habari hizi"

Ndugu zake

"Waumini wengine"

Acts 12:18

Sasa

Hili limetumika kutenganisha simulizi. Muda umekwishapita, sasa ni siku nyingine.

Kulipokuwa mchana,

"Saa ya asubuhi"

kukawa na huzuni kubwa

Kinyume cha huzuni kubwa ni "Furaha kubwa" Askari hao hawakuwa na furaha hiyo tena.

Furaha kubwa

Hili linaelezea kinyume cha furaha kama; Msongo wa mawazo, mashaka, hofu na kuchanganyikiwa.

kuhusu

"Kuhusiana na"

Baada ya Herode kumtafuta na hakumwona

"Herode alimtafuta Petro na kushindwa kumpata"

akawauliza walinzi na akaamuru wauawe

Ilikuwa ni adhabu ya kawaida kwa serikali ya Rumi kuua walinzi kama mfungwa wao aliwatoroka.

Akaenda kutoka uyahudi mpaka Kaisaria

Kaisaria ilikuwa chini zaidi ya Yudea.

Acts 12:20

Sentensi unganishi

Luka anaendelea na simlizi nyingine juu ya maisha ya Herode.

Sasa

Neno linaloweka daraja la kuelekea kwenye tukio jingine.

Wakaenda kwa pamoja kwake.

Ni tukio lisilofurahisha kwamba wote walikwenda kwa Herode. "Wanaume waliowawakilisha watu wa Tiro na Sidoni walienda kwa pamoja kufanya mazungumzo pamoja na Herode.

Wakawa na urafiki na Blasto

"Hawa watu walimfanya kuwa rafiki yao"

Blasto

Blasto alikuwa msaidizi au ofisa wa Mfalme Herode.

wakaomba amani,

"Wanaume wale waliomba kuwe na amani"

nchi yao ilipokea chakula kutoka katika nchi ya mfalme.

Yawezekana walinunua chakula hiki. "Watu wa Tiro na Sidoni walikuwa wakinunua chakula chao chote kutoka kwa watu waliotawaliwa na Herode."

nchi yao ilipokea chakula

Inaonekana Herode alikuwa amezuia nchi yake kutoa chakula kwa Tiro na Sidoni kwasababu alikuwa amewakasirikia watu wa nchi hizo.

Siku iliyokusudiwa

Hii inawezekana ilikuwa ni siku ambayo Herode alikubali kukutana na wawakilishi wa miji ya Tiro na Sidoni.

mavazi ya kifalme

Mavazi ya gharama ambayo yangemdhihirisha kuwa alikuwa mfalme.

kukaa kwenye kiti chake cha kifalme,

Hii ilikuwa ni kawaida ya Herode kufanya wakati watu walikuja kumwona.

Acts 12:22

Sentensi unganishi

Hii ni sehemu ya mwisho ya simlizi ya Mfalme Herode.

Ghafla

"Wakati huo huo" au "Wakati watu walipokuwa wakimsifia Herode"

akampiga,

"Herode aliharibiwa" au " kikasababisha Herode kuwa mgonjwa sana"

hakumpa Mungu utukufu

Herode akawaruhusu watu wamwabudu yeye badala ya kuwaambia wamwabudu Mungu.

akaliwa na chango na akafa

"Chango" inaonyesha na wadudu ndani ya mwili, labda minyoo katika utumbo.

Acts 12:24

Maelezo ya jumla

Hii ni taarifa inayotoa mrejesho juu ya kuenea kwa neno la Mungu na kwa vile Barnaba na Sauli walikuwa wakifanya.

neno la Mungu likakua na kusambaa

Neno la Mungu likahubiriwa kama vile mti mbichi uliokuwa na uwezo wa kustawi na kuzaa matunda. "Neno la Mungu likasambaa katika maeneo mbalimbali na watu wakamwamini."

Neno la Mungu

Watu wengi walisikia habari za neno la Mungu na kuupokea wokovu kwa njia ya Yesu.

kukamilisha huduma yao wakatoka pale wakarejea Yerusalemu,

Inaelezea wakati walipopeleka fedha kutoka kwa waumini wa Antiokia sura 11:29.

walirudi kutoka kule

Walirudi kwenda Antiokia. "Baraba na Sauli walirudi Antiokia"

wakamchukua na Yohana

"Baraba na Sauli walimchukua Yohana pamoja nao"

ambaye jina la kuzaliwa ni Marko

"Alikuwa akiitwa jina jingine Marko"

Acts 13

Matendo 13 Maelezo kwa jumla

Muundo na Mpangilio

Tafsiri zingine zimeweka nukuu kutoka Agano La Kale kwenye mkono wa kulia mbali na maandiko mengine. ULB hufanya hivi kwa kutumia nukuu tatu kutoka Zaburi 13:33-35

Tafsiri zingine zimeweka kila mstari wa ushairi mbele ya kulia kuliko maandishi mengine ili kurahisisha kusoma. ULB hufanya hiv na ushairi ambao umenukuliwa kutoka Agano la Kale 13:41

Nusu ya pili ya kitabu cha Matendo inaanzia katika sura hii. Luka anaandika zaidi kumhusu Paulo kuliko Petero, na inelezea jinsi watu wa mataifa, na siyo Wayahudi, wanafunuliwa habari ya Yesu na waumini.

Dhana Maalum katika sura hii.

Mwanga kwa watu wa mataifa

Mara nyingi Biblia huzungumzia watu wasio wanyoofu, watu wasiotenda yanayomfurahisha Mungu,kana kwamba ni watu watembeayo kwa giza. Inazungumzia mwanga kana kwamba ndio unaweazesha wenye dhambi kubadilika ili wafahamu kwamba wanachotenda ni kibaya na waanze kumtii Mungu. Wayahudi waliwachukulia watu wote wa mataifa kama watembeao kwa giza lakini Paulo na Barnaba wakazungumzia watu wa mataifa kumhusu Yesu kama watakaoenda kuwaletea mwanga wa kawaida. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous) Jesus as if they were going to bring them physical light. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/jit.html#figs-metaphor and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous)

<< | >>

Acts 13:1

Sentensi unganishi

Luka anaanza kuzungumzia habari za safari za huduma ambazo kanisa la Antiokia liliwatuma Barnaba na Sauli.

Maelezo ya jumla

Mstari wa 1 unatupatia maelezo kuhusu watu wa kanisa la Antiokia.

Sasa katika kanisa la Antiokia,

"Kwa wakati, kanisa la Antiokoa"

Simeoni (aliyeitwa Nigeri). Lukio wa Kirene, Manaen

"Majina ya baadhi ya waliokuwepo katika kanisa la Antiokia

ndugu asiye wa damu wa Herode kiongozi

"Manaeni alikuwa pengine rafiki yake na Herode waliocheza michezo ya ujana pamoja naye"

kiongozi wa mkoa

"Mtawala wa sehemu au robo ya nchi"

Wakati

Neno hili linatambulisha matukio mawili yaliyokuwa yanatendeka kwa wakati mmoja.

Niteengeeni pembeni

"Nitengeeni hao kwa kunitumikia mimi"

kazi niliyo waitia.

Linamaanisha, Mungu amewachagua kufanya hazi hii.

na kuweka mikono yao juu ya watu hawa

"Wakaweka mikono juu ya manaume hao ambao Mungu alikuwa amejitengea kwa kazi yake. Tendo hili lilionyesha kwamba viongozi walikubali kuwa Roho Mtakatifu alikuwa amewaita Barnaba na Sauli kwa kuifanya kazi hii."

wakawaacha waende.

"Wakawaacha waende zao" au "Wakawatuma wanaume hao kutenda kazi ambayo Roho Mtakatifu alikuwa amewatuma kuitenda"

Acts 13:4

Maelezo ya jumla

Luka anandika kuwaelezea Barnaba na Sauli

Sasa

Neno hili linatambulisha tukio lililotendeka kwasababu ya lile lililokuwa limetangulia kutukia. Tukio la mwanzo lilikuwa la kutengwa na Roho Mtakatifu kwa Barnaba na Sauli

walitelemka

Neno "Kutelemka" linatumika hapa kwasababu Seleukia ni mji ulio chini zaidi ya Antiokia.

Seleukia

Mji ulio kandokando ya ziwa.

Mji wa Salami

Mji wa Salami ulikuwa katika kisiwa cha Kipro.

Sinagogi la Wayahudi

Maana inayowezekana; 1) "Kulikuwa na masinagogi mengi ya Wayahudi katika mji wa Salami mahali Barnaba na Sauli walihubiri" au 2) Barnaba na Sauli waliaza kuhubiri ndani ya Sinagogi katika mji wa Salami na kuendelea kuhubiri katika Masinagogi waliyoyaona wakati wakisafiri kuzunguka kisiwa hicho cha Kipro

walikuwa pamoja na Yohana Marko kama msaidizi wao.

"Yohana Marko alisafiri pamoja nao na alikuwa akiwasaidia"

Msaidizi

"Aliyewahudumia"

Acts 13:6

Maelezo ya jumla

Mistari hii imetaja viwakilishi vingi vya majina kuelezea watu mbalimbali walio tajwa na mwandishi Luka.

katika kisiwa chote

Walitembelea kisiwa chote kutoka upande mmoja hadi upande mwingine wakiunena ujumbe wa Injili katika kila mji walimopita.

Pafo

Ni mji Mkuu wa kisiwa cha Kapro mahali Liwali alikuwa akiishi.

Walimkuta

Neno "Kumkuta" linamaanisha kuwa walimfikia bila ya kumtafuta.

Mtu fulani mchawi

"Mtu aliyekuwa akifanya kazu ya uchawi" au "Mtu aliyekuwa akifanya mambo yasiyo ya kawaida katika fani ya kimazingaombwe"

ambaye jina lake lilikuwa Bar Yesu

"Bar - Yesu" maana yake "Mwana wa Yesu". Hakukuwa na mahusiano yoyote ya karibu na Yesu Kristo". Jina Yesu lilikuwa ni jina la kawaida katkia wakati ule.

Mchawi huyu alishirikiana

"Alikuwa mara kwa mara pamoja na" au "Alikuwa mara kwa mara akiambatana na"

Liwali

Huyu alikuwa Kiongozi mtendaji Katika utawala mkoa wa dola ya Rumi.

aliyekuwa mtu mwenye akili

Hii ni historia ya maisha ya Liwali Sergio Paulus.

Lakini Elima "yule mchawi"

Huyu alikuwa Bar- Yesu, ambaly aliyekuwa akiitwa mchawi.

hivyo ndivyo jina lake lilivyo tafsiriwa

"Hivyo ndivyo jina lake katika lugha ya kigriki"

aliwapinga; alijaribu kumgeuza

"Aliwazuia akijaribu kumgeuza"

alijaribu kumgeuza yule liwali atoke kwenye imani

"Alijaribu kumshawishi Liwali kuiacha imani ya ujumbe wa Injli"

Acts 13:9

Sentensi unganishi

Wakati wakiwa katika kisiwa cha Pafo, Pauli alianza kuzungumza na Elima.

Lakini Sauli aliyeitwa Paulo

"Sauli" ambalo ni jina la Kiyahudi, na "Paulo" ambalo ni jina la Kirumi. Wakati alipokuwa akizungumza na mtawala wa Rumi, alikuwa akitumia jina la Kirumi.

akamkazia macho

"Akamkazia macho kwa makini"

Ewe mwana wa Ibilisi

Paulo anasema yule mtu alikuwa akitenda kama Ibilisi. "Wewe sawa na shetani" au "Unatenda kama Shetani"

umejazwa na aina zote za udanganyifu na uovu

"Wakati wote unatenda kwa kusababisha wengine waamini ambacho si kweli kwa kutumia udanganyifu na mara zote unatenda mabaya"

Uovu

Inamaanisha kuwa mzembe na kutokufuata sheria ya Mungu kwa dhati.

Wewe ni adui wa kila aina ya haki

Paulo anamwunganisha Elima pamoja na Ibilisi. Kama vile Ibilisi ni adui wa Mungu kwa kuwa kinyume na haki, ndivyo ilivyo kwa Elima pia.

Hautakoma kuzigeuza njia za Bwana, zilizonyooka, je utaweza?

Paulo anatumia swali kumkemea Elima kwa upinzani wake kwa Mungu.

njia za Bwana, zilizonyooka

Hapa "njia zilizonyoka" linamaanisha njia zilizo za kweli katika Bwana.

Acts 13:11

Sentensi unganishi

Paulo anamalizia majadiliano na Elima.

mkono wa Bwana upo juu yako

Neno "mkono" unawakilisha nguvu za Mungu na neno "juu yako" linamaanisha adhabu . "Mungu atakuadhibu"

utakuwa kipofu.

Hii inaweza kutafsiriwa kuwa; "Mungu atakufanya kipofu"

Hautaliona Jua

Elima atakuwa kipofu kabisa kwamba hataweza kuliona jua.

kwa muda

"Kwa kipindi fulani" au "Mpaka muda wa Mungu aliouamru"

mara moja ukungu na giza vilianguka juu ya Elimas

"Macho ya Elima yakapata ukungu na giza" au "Elima uoni ulikuwa hafifu na kisha hakuweza kuona kabisa"

alianza kuzunguka pale

"Elima alianza kutangatanga"

Liwali

Huyu alikuwa ni mtumishi wa serikali katika jimbo la Rumi.

Aliamini

"Alimwamini Yesu"

alishangazwa kwa mafundisho kuhusu Bwana.

"Mafundisho kuhusu Bwana Yesu yalimshangaza mno"

Acts 13:13

Sentensi unganishi

Hii ni sehemu mpya ya simlizi kuhusu Paulo akiwa Antiokia ya Pisidia

Maelezo ya jumla

Mistari ya 13 na 14 inatupa inatupa ufafanuzi wa simlizi hiyo.

Maelezo ya jumla

"Paulo na rafiki zake" Walikuwa Barnaba na Yohana Marko (aliyeitwa Yohana). Kutokea hapa na kuendelea, Sauli akaitwa Paulo katika Matendo ya Mitume. Jina la Paulo limeorodheshwa kwanza kuonyesha kuwa alikuwa kiongozi wa kundi. Ni muhimu kutunza mtiririko huu katika tafasiri.

Sasa

Linaonyesha mwanzo wa kipengere na simlizi mpya.

walisafiri majini kutoka Pafo

"Walisafiri kwa kutumia jahazi kutoka Pafo"

wakafika Perge katika Pamfilia.

"Walifika Perge iliyo Pamfilia"

Lakini Yohana aliwaacha

"Lakini Yohana Marko akawaacha Paulo na Barnaba"

Antiokia ya Pisidia.

"Mji wa Antiokia ni wilaya ya Pisidia"

Baada ya kusoma sheria

"Sheria na Manabii" Inamaanisha sehemu ya maandiko ya Wayahudi ambayo yalisomwa. 'Baada ya mtu mmoja kusoma kutoka vitabu vya sheria na maandiko ya Manabii"

waliwatumia ujumbe wakisema

"Wakiwaomba mmoja wao aseme neno"

Ndugu

Neno "ndugu" lilitumika wa watu katika Sinagogi kuwazungumzia Paulo na Barnaba kama Wayahudi wenzao.

kama mnao ujumbe wa kutia moyo

"Kama mnataka kutuambia jambo lolote la kututi moyo"

semeni

"Tafadhali mnaweza kunena"

Acts 13:16

Sentensi unganishi

Paulo anaanza hotuba yake kwa watu waliokuwamo kwenye Sinagogi huko Antiokia ya Pisidia. Anaanza kwa kuzungumzia mambo ambayo yalitokea katika historia ya Israeli.

alisimama na kuwapungia mkono

Inamaanisha kutoa ishara kwa mikono kwamba yuko tayari kuanza kusema.

enyi mnao mtii Mungu

Anamaanisha, Wamataifa ambao wanafuata desturi na dini ya Kuyahudi. "Ninyi msio Waisrael, lakini mnamwabudu Mungu"

sikilizeni

"Nisikieni mimi" au "Sikieni ambacha nataka kuwaambia"

Mungu wa hawa watu wa Israeli

"Mungu ambye anaabudiwa na Waisraeli

baba zetu

"Mababa wa Wayahudi"

na kuwafanya watu wengi

"Aliwawezesha wao kuwa watu wengi sana"

kwa mkono wake kuinuliwa

anamaanisha Mkono wa Mungu wenye uweza.

aliwaongoza nje yake

"Kutoka katika nchi ya Misri"

aliwavumilia

linamaanisha "Aliwajali" na "Aliwavumilia katika kutokutii kwao"

Acts 13:19

Maelezo ya jumla

Mwinjilisti Luka katika kuandika kwake anatumia viwakilishi vingi vya majina kuelezea wale ndugu wanaotajwa katika vifungu hivi.

Mataifa

Neno "Mataifa" linafafanua tofauti ya makundi ya watu na siyo mipaka ya mataifa kijiografia.

yalitokea zaidi ya miaka mia nne na hamsini

lichukua muda wa miaka mia nne na hamsini kuikamilisha kazi ya kuyaondoa mataifa Kanaani.

mpaka Samweli Nabii

"Muda huo ulifikia hata kipindi cha Nabii Samweli"

Acts 13:21

Maelezo ya jumla

Nukuu katika simlizi hii inatoka katika kitabu cha Samweli na katika Zaburi za Ethani katika Agano la kale.

kwa miaka arobaini

"Kuwa mfalme wao kwa miaka arobaini"

kumuondoa katika ufalme

Inamaanisha kuwa Mungu alisababisha Sauli asiendelee kuwa Mfalme. "Alimkataa asiwe Mfalme"

alimwinua Daudi kuwa mfalme wao

"Mungu alimchagua Daudi kuwa Mfalme wao."

Mfalme wao

"Mfalme wa Israeli" au "Mfalme juu ya Waisreli"

Ilikuwa ni kuhusu Daudi kwamba Mungu alisema

"Mungu alisema hivyo kuhusu Daudi"

Nimempata

"Nimeshaona kwamba"

kuwa mtu apendezwaye na moyo wangu

namaanisha kuwa "Yeye ni mtu anayetaka kutenda ambayo mimi nataka"

Acts 13:23

Maelezo ya jumla

Nukuu hii inatoka katika vitabu vya Injili.

Kutoka kwenye ukoo wa mtu huyu

"KUtoka katika ukoo wa Daudi." Hii imewekwa mwanzoni mwa sentensi kuelezea kuwa Mwokozi angekuwa nduye aliyetoka katika ukoo wa Daudi.

ameiletea Israeli

Inamaanisha watu wa Israeli.

kama alivyoahidi kufanya

"Kama vile Mungu alivyoahidi angefanya"

Ubatizo wa toba

Unaweza kulitafasiri neno "toba" kama kitenzi kama vile; "Ubatizo kwa watu waliotakiwa kutubu kwa ajili ya dhambi zao."

"Mwanifikiri mimi ni nani?"

Yohana aliuliza swali kuwafanya watu wafikirie Yohana alikuwa nani.

mimi si yule

Yohana alikuwa anamwelezea Masihi, ambaye watu walikuwa wanamtegemea kuja.

Lakini sikilizeni

Neno linalo elezea umuhimu wa kile ambacho atakwenda kusema.

ajaye nyuma yangu

Hii pia inazungumzia kuja kwa Masihi. "Masihi atakuja Mapema"

sisitahili kulegeza viatu vya miguu yake.'

"Mimi sistahili hata kungua kamba za kiatu chake."

Acts 13:26

Maelezo ya jumla

Viwakilishi vya majina hapa vinamuwakilisha Paulo na kundi lote la watu waliokuwemo kwenye Sinagogi.

Ndugu, watoto wa ukoo wa Abrahamu, na wale ambao kati yenu mnamwabudu Mungu

Paulo analielezea kundi la Wayahudi na wale wa mataifa walioungia katika dini ya kiyahudi ili kubaki na hali yao waliyoichagua ya kumwabudu Mungu wa kweli.

ujumbe huu wa ukombozi umetumwa

Kwa maneno mwngine; "Mungu ameshatuma ujumbe wake wa wokovu"

Ukombozi huu

Neno hili linamaanisha kwamba; "Mungu atawaokoa watu"

hawakumtambua

"Hawakuweza kabisa kumtambua huyu mtu Yesu alikuwa ni mmoja ambaye Mungu alimtuma kuwakomboa."

Ujumbe wa manabii.

Unawakilisha; "Maandiko ya manabii" au "Ujumbe wa manabii."

ambao unasomwa

"Ambao mtu anausoma"

walitimiliza ujumbe wa manabii

"Hakika walitenda kama vile Manabii walivyosema."

Acts 13:28

Maelezo ya jumla

Viwakilishi vya majina, vinawakilisha Wayahudi na Viongozi wa dini zao katika Yerusalemu.

hawakupata sababu nzuri kwa kifo ndani yake

"Hawakupata sababu zenye maana kwanini Yesu alipaswa auawe"

Walimwomba Pilato amwue

Neno "Kumwomba" ni neno lenye nguvu likimaanisha "Kutaka, kulazimisha, kudai"

Walipomaliza mambo yote yaliyoandikwa kuhusu yeye

"Wakati walipomtendea Yesu, kila kitu walichokuwa wamekisema manabii kilitimia.

walimshusha kutoka mtini

"Walimwua Yesu na kuuondoa mwili wake kutoka kwenye msalaba baada ya kufa."

kutoka mtini

"Kutoka msalabani"

Acts 13:30

Lakini Mungu alimfufua

"Lakini" ni neno linaloonyesha nguvu ya kutofautisha usemi uliotangulia na ule unaofuata kama vile; "Watu walimwua Yesu lakini Mungu alimfufua Yesu"

alimfufua kutoka wafu.

"Alimfufu kutoka miongoni mwa wale waliokuwa wamekufa"

kufufuliwa

"Kufanywa mzima tena"

Alionekana... Galilaya kuelekea Yerusalemu.

"Wanafunzi waliotembea pamoja na Yesu kutoka Galilaya mpaka Yerusalemu wakimwona kwa siku nyingi."

Siku nyingi

"Tunajua kutoka maandiko mengine kwamba, muda wa siku arobaini"

hawa sasa ni mashahidi wa watu.

"Sasa wanashuhudia kwa watu habari za Yesu"

Acts 13:32

Maelezo ya jumla

Nukuu ya pili hapa inatoka katika kitabu cha nabii Isaya.

Hivyo

Kiunganishi cha neno kinachoonyesha tukio kwamba tukio lililokwisha kupita ni kwasababu ya tukio lililokuwa limetangulia kutukia. Tukio la nyuma kabla ya lile lililofuata ni la kumfufua Yesu kutoka kwa wafu.

mababu zetu.

"mababu zetu" Paulo bado anaongea na Wayahudi na watu wa mataifa waliofuata desturi za Kiyahudi huko Antiokia Pisidia. Hawa walikuwa mababu wa kimwili wa Wayahudi na Mababu wa kiroho wa wakristo wa mataifa waliofuata desturi za Kiyahudi.

Mungu aliweka ahadi hizi

"Mungu amekwisha timiza hizo ahadi"

kwetu, watoto wao,

"Kwetu" inamaanisha wale watoto wa hao mababu"

katika hilo alimfufua Yesu na kumrudisha tena katika uhai

"Kwa kumfanya Yesu kuwa mzima tena"

Hili pia liliandikwa katika Zaburi

kweli huu umeandikwa pia na Zaburi ya pili."

Mwanangu, leo nimekuwa Baba yako

Hivi ni vyeo muhimu vinavyoeleza ule uhusiano kati ya Yesu na Mungu.

kwamba alimfufua kutoka wafu ili kwamba mwili wake usiharibike, ameongea hivi

"Mungu alinena haya maneno juu ya kumfanya Yesu kuwa mzima tena ili asionekane na mauti tena"

Kutoka kwa wafu

"Wafu" ni neno linalowakilisha watu waliokwisha kufa. Atamfufua kutoka miongoni mwao na kumfanya kuwa mzima tena"

baraka halisi

"Baraka za kipekee"

Acts 13:35

Hii ndiyo sababu kasema pia katika zaburi nyingine

Wasikilizaji wa Paulo wangeweza kufahamu kuwa Zaburi hii ilikuwa inamtaja Masihi.

Anasema pia

"Daudi pia alisema." Daudi ni mwandishi wa Zaburi ya 16 ambapo nukuu hii imechukuliwa.

'Hautaruhusu mtakatifu wako kuuona uozo.'

Neno "kuona uozo" ni neno linalofanana na "kuharibika." Hutaruhusu mwili wa mtakatifu wako kuharibika."

Hutaruhusu

Hapa Daudi anamwambia Mungu.

Katika kizazi chake

"Katika kipindi cha uhai wake"

kutumika katika nia ya Mungu

"alifanya kile alichomtaka Mungu kufanya"

alilala,

Hii ilikuwa lugha laini iliyokwa inazungumzia kifo.

alilazwa pamoja na baba zake

"Alizikwa pamoja na baba zake waliokuwa wamekufa"

aliuona uaharibifu

"Kuona uharibifu" ni kusema kuwa "Mwili wake uliharibiwa"

Lakini aliyefufuliwa

"Lakini Yesu ambaye"

hakuuona uharibifu

"Yesu hakuona uharibifu"

Acts 13:38

Maelezo ya jumla

Kiwakilishi cha jina "yeye" linaelezea juu ya Yesu.

na ifahamike kwenu

"Fahamu hivi" au "Hii ni muhimu kwako kujua"

Ndugu

Paulo anatumia lugha ua ndugu kuona Wayahudi na wafuasi wa dini ya kiyahudi wote ni ndugu.

ifahamike kwenu, ndugu, kupitia mtu huyu, msamaha wa dhambi

"tunawatangazia kuwa dhambi zenu zinaweza kusamehewa kupitia Yesu."

Msamaha wa dhambi

"Msamaha" inaweza kutafasiriwa kuwa; Mungu anaweza kusamehe dhambi zako"

Kwa yeye kila aaminiye

"Kila mmoja anayemwamini yeye"

Kwa yeye kila aaminiye anahesabiwa haki

"Yesu anamhesabia haki kila mmoja anayemwamini"

Kila kitu

"dhambi zote"

Acts 13:40

Sentensi ungsnishi

Paulo anamalizia hotuba yake katika Sinagogi la Antiokia ya Pisidia aliyoianza katika sura 31:16.

Maelezo ya jumla

Katika ujumbe wake kwa watu wa Sinagogi, Paulo ananukuu nukuu ya Nabii Habakuki.

Kuweni waangalifu

"Iweni waangalifu kwa mambo ambayo nimekwisha waelezeni."

kwamba kitu walichokiongelea manabii

"Kwa kile manabii walishawahi kuzungumzia"

Tazama, enyi mnaodharau

"Mnaofanya mizaha, dharau"

mkashangae

"Mkashitushwe"

mkaangamie

"Kisha kufa"

Ninafanya kazi

"Ninatenda kitu"

Katika siku zenu

"Kipindi cha uhai wenu"

Kazi ambayo

"Ninafanya kitu ambacho"

hata kama mtu atawaeleza."

"Hata ikiwa mtu mmoja kuwaanbia habari yake"

Acts 13:42

Paulo na Barnaba walipoondoka

"Wakati Paulo na Barnaba walipokuwa wakiondoka"

wakawaomba waongee

"Wakawaomba"

Maneno yale yale

"Maneno ambayo Paulo alikuwa ameyatamka kwenye hotuba yake"

Wakati mkutano wa sinagogi ulipokwisha

Inaweza kuwa; 1) Wakati Paulo na Barnaba walipoondoka mstari 42: au 2) Paulo na Barinaba waliopouacha mkutano kabla ya kuhitimisha.

Wongofu

"Hawa walikuwa si Wayahudi ambao hawakufuata utamaduni wa Kiyahudi"

waliongea nao na waliwahimiza

"Na Paulo na Barnaba walinena nao hao na kuwasihi"

waendelee katika neema ya Mungu.

"Waendelee kumtumaini Mungu ambaye husamehe dhambi kwasababu ya kile Yesu alifanya kwao"

Acts 13:44

Karibu mji mzima

"Mji" Ni neno linaliwakilisha watu wa mji huo.

kusikia neno la Mungu.

"Kuwasikia Paulo na Barnaba wakinena neno la Bwana Yesu.

Wayahudi

:Hawa ni Wayahudi Viongozi"

walijawa na wivu

"Hali ya wivu ikawajia"

Wakaongea masneno ya kupinga

"Maneno yaliyopinga ujumbe wao"

maneno yaliyopinga vitu vilivyosemwa na Paulo

"Mambo yale yaliyosemwa na Paulo"

Acts 13:46

Maelezo ya jumla

Paulo ananukuu nukuu ya Nabii Isaya katika Agano la Kale.

Ilikuwa ni muhimu

"Mungu alikuwa ameagiza kile cha kufanya"

kwamba neno la Mungu liongelewe kwanza kwenu

"Kwamba tulinene neno la Mungu kwenu kwanza"

kuwa mnalisukumia mbali kutoka kwenu

"Kulipinga neno la Mungu lililonenwa"

nakujiona kuwa hamkusitahili uzima wa milele

Mmeonyesha kuwa hamkuuthamini uzima wa milele"

tutawageukia Mataifa.

"Tutawaambia watu wa Mataifa habari za Yesu"

kama nuru

Hapa ni ukweli kuhusu Yesu kwamba Paulo alikuwa akihubiri kana kwamba kulikuwa na nuru iliyokuwa ikiruhusu watu kuona.

kwamba mlete wokovu kwa pande zote za dunia

"Kuwaambia watu mahali pote katika dunia kwamba ninataka kuwaokoa"

Acts 13:48

kulisifu neno la Bwana.

"Kumsifu Mungu kwa ujumbe kuhusu Bwana Yesu"

Wengi waliochaguliwa kwa uzima wa milele

"Watu wote ambao Mungu alikuwa amewachagua kupokea uzima wa milele"

Neno la Bwana lilienea nchi yote

"Wale alioliamini jina la Yesu walienda kila mahali katika jimbo hilo na kuwaambia wengine habari za Yesu"

Acts 13:50

Sentensi unganishi

Huu ni muda wa mwisho wa Paulo na Barnaba kukaa Antiokia ya Pisidia na wakaenda ikonia.

Wayahudi

Hii yawezekana kuzungumzia viongozi wa Kiyahudi.

Waliwasihi

"Kushawisha" au "kuhamasisha"

Wanaume viongozi

"Wanaume mashuhuri"

Haya yalichochea mateso dhidi ya Paulo na Barnaba

"Walishawishi wanaume mashuhuri na wanawake kuwatesa Paulo na Barnaba"

waliwatupa nje ya mipaka ya mji.

"Waliwatoa Paulo na Barnaba kutoka nje ya mji"

walikung'uta mavumbi ya miguu yao.

"Huu ulikuwa tukio la mfano kuonyesha kwa watu wasioamini kwamba Mungu alikuwa amewakataa na angeweza kuwahukumia"

Wanafunzi

"Yawezekana ni wale waumini wapya walioamini huko Antiokia Pisidia ambao Paulo na Barnaba waliwaacha"

Acts 14

Matendo 14 Maelezo kwa jumla

Dhana Maalum katika sura hii

"Ujumbe wa neema yake"

Ujumbe wa Yesu ni ujumbe wa Mungu ambao huwapa neema wanaomuamini Yesu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#grace and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#believe)

Zeu na Herme

Watu wa mataifa katika himaya ya Warumi waliabudu miungu wengi ambao hawakuwepo. Paulo na Barnaba waliaambia kuamini katika "Mungu aliye hai" Yahwe. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#falsegod)

Maswala mengine tata kwenye tafsiri ya sura hii.

"Lazima tuingie kwenye ufalme wa Mungu kupitia mateso mengi"

Yesu aliwaambia wafuasi wake kabla hajafa kwamba kila anayemfuata angepata mateso. Paulo anayarudia maneno hayo kupitia maneno tofauti na hayo.

<< | >>

Acts 14:1

Maelezo ya jumla

Habari ya Paulo na Barnaba Ikonia inaendelea.

Ikatokea katika Ikonia ya kwamba

Maana hapa yawezekana kuwa 1) "ilitokea Ikonia ya kwamba" au 2) "Kama kawaida ndani ya Ikonia"

alizungumza kwa namna ambayo

"alizungumza kwa namna ambayo." Inaweza kusaidia kutamka kwamba walizungumza ujumbe kuhusu Yesu. "walizungumza ujumbe kuhusu Yesu kwa nguvu"

Wayahudi waliokuwa hawatii

Hii inalenga kikundi cha Wayahudi ambao hawakumuamini ujumbe wa Yesu.

kutikisa akili za Wayunani

kusababisha Wayunani kuwa na hasira inazungumzwa kana kwamba maji yaliyotulia kuchafuliwa.

akili

hapa neno "akili" linamaanisha watu

ndugu

hapa "ndugu" linamaanisha Paulo na Barnaba na waumini wapya.

Acts 14:3

Maelezo ya jumla

Hapa neno "Yeye" linamaanisha Bwana.

Kwa hiyo wakabaki kule

"Hata hivyo walibaki kule." Paul na Barnaba walibaki ikonia kuwasaidia watu wengi walioamini katika 14:1. "Kwa hiyo" inaweza kuondolewa kama itaongeza mchanganyiko kwenye maandishi.

kutoa uthibitisho kuhusu ujumbe wa neema yake

"kuonesha kwamba ujumbe kuhusu neema yake ni kweli"

kuhusu ujumbe wa neema yake

"kuhusu ujumbe wa neema ya Bwana"

kwa kuruhusu ishara na maajabu kufanywa na mikono ya Paulo na Barnaba.

HIi inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "kwa kuwawezesha Paulo na Barnaba kufanya ishara na maajabu"

kwa mikono ya Paulo na Barnaba

Hapa "mikono" inamaanisha nia na juhudi za wanaume hawa wawili kulingana na walivyoongozwa na Roho Mtakatifu. "kwa huduma ya Paulo na Barnaba"

sehemu kubwa ya mji uligawanyika

Hapa "mji" inamaanisha watu waliomo kwenye mji. "watu wengi wa mji waligawanyika" au "watu wengi wa mji hawakukubaliana"

walikuwa upande wa wayahudi

"waliaunga mkono Wayahudi" au "walikubaliana na Wayahudi." Kundi la kwanza lililotajwa halikukubaliana na ujumbe kuhusu neema.

na mitume

Kundi la pili lililotajwa lilikubaliana na ujumbe kuhusu neema. Inaweza kusaidia kutaja tena kitezi. "walijiunga na mitume"

mitume

Luka anamaanisha Paulo na Barnaba. Hapa "mitume" inaweza kutumika katika hali ya ujumla ya "wale waliotumwa nje."

Acts 14:5

Taarifa ya Jumla:

Hapa waliopata habari ni Paulo na Barnaba.

walijaribu kuwashawishi viongozi wao

"walijaribu kuwashawishi viongozi wa Ikonio." Hapa "walijaribu" inaashiria hawakuweza kuwashawishi kikamilifu kabla ya mitume kuondoka katika mji.

kuwatesa na kuwapiga mawe Paulo na Barnaba

"kuwapiga Paulo na Barnaba na kuwaua kwa kuwaponda mawe"

Likaonia

Wilaya ndani ya Asia Ndogo

Listra

Mji ndani ya Asia Ndogo kusini mwa Ikonio na Kaskazini mwa Derbe

Derbe

Mji ndani ya Asia Ndogo kusini mwa Ikonio na Listra

huko walikuwa wakihubiri injili

"Paulo na Barnaba walihubiri injili pia huko"

Acts 14:8

Kauli Unganishi:

Paulo na Barnaba sasa wako Listra.

Taarifa ya Jumla:

Taarifa ya Jumla: Anayezungumziwa kuwa na imani ni yule kiwete; na aliyemsemesha ni Paulo. Yule aliyesemeshwa ni kiwete.

mtu fulani aliketi

Hii inatambulisha mtu mpya katika simulizi.

dhaifu miguuni mwake

"kutokuweza kusogeza miguu yake" au "kutokuweza kutembea kwa miguu yake"

kiwete

"kilema"

kiwete tangu tumboni mwa mama yake

"kiwete tangu kuzaliwa"

Paulo alimkazia macho

"Paulo alimtazama moja kwa moja"

alikuwa na imani ya kufanywa mzima

Nomino "imani" inaweza kutafsiriwa kama kitenzi "amini." "aliamini kwamba Yesu anaweza kumponya" au "aliamini kuwa Yesu anaweza kumfanya mzima"

akaruka juu

"akaruka hewani." Hii inaashiria kwamba miguu yake ilikuwa imeponywa kikamilifu.

Acts 14:11

alichokifanya Paulo

Hii inamaanisha uponyaji wa Paulo kwa kiwete.

miungu imeshuka kwetu

Idadi kubwa ya watu iliamini kuwa Paulo na Barnaba walikuwa miungu ya kipagani walioshuka toka mbinguni. "miungu wameshuka toka mbinguni kuja kwetu"

katika lahaja ya Likaonia

"katika lugha yao ya Kilikaonia" (UDB). Watu wa Listra walizumngumza Kilikaonia na Kigriki pia.

katika mfano wa mwanadamu

Watu hawa waliamini kuwa miungu walihitaji kubadili mionekano yao ili wawe kama binadamu.

walimuita Barnaba "Zeu"

Zeu alikuwa mfalme juu ya miungu wengine wote wa kipagani.

Paulo, Herme, kwa sababu alikuwa msemaji mkuu

Herme alikuwa mungu wa kipagani aliyeleta ujumbe kutoka kwa Zeu na miungu wengine.

Kuhani wa Zeu, ambaye hekalu lake lilikuwa nje tu ya mji, alileta

Inaweza kusaidia kuweka taarifa ya ziada kuhusu kuhani. "Kulikuwa na hekalu nje tu ya mji ambapo watu walimwabudu Zeu. Kuhani aliyehudumu katika hekalu aliposikia kile ambacho Paulo na Barnaba walichokifanya, alileta

ng'ombe na mashada ya maua

Ng'ombe walikuwa ni wakutolewa sadaka. Mashada yalikuwa mojawapo kati ya kuwawekea mataji Paulo na barnaba, au kuwawekea ng'ombe kwa ajili ya sadaka.

milangoni

Milango ya miji mara nyingi ilitumika kama sehemu ya kukutana kwa watu wa mji husika.

walitaka kutoa sadaka

"walitaka kutoa sadaka kwa Paulo na Barnaba kama miungu Zeu na Herme.

Acts 14:14

mitume, Barnaba na Paulo

Inawezekana Luka anatumia "mtume" katika hali ya ujumla ya "yule ambaye ametumwa."

walichana nguo zao

Hili ni tendo la ishara kuonesha kuwa walihuzunishwa na kukasirishwa kwamba kundi lilitaka kuwatolea wao sadaka.

Watu, kwa nini mnafanya hivi vitu?

Barnaba na Paulo wanawakaripia watu kwa kujaribu kuwatolea sadaka. "watu, hampaswi kutuabudu!"

Sisi pia ni binadamu wenye hisia kama nyie

Kwa kauli hii, Baranaba na Paulo wanasema kuwa wao sio miungu. "Sisi ni binadamu tu kama nyie.. Sisi sio miungu!"

wenye hisia sawa na nyie

"kama nyie kwa kila hali"

mgeukieni Mungu aliye hai kutoka kwa vitu hivi visivyo na maana

"acheni kuabudu miungu ambayo haiwezi kuwasaidia, na badala yake anzeni kumuabudu Mungu aliye hai"

Mungu aliye hai

"Mungu ambaye kweli yupo" au "Mungu anayeishi"

Siku za nyuma

"katika nyakati za zamani" au "Hadi sasa"

kutembea katika

"kuishi kulingana na"

Acts 14:17

Kauli Unganishi:

Paulo na Barnaba wanaendelea kuzungumza na kundi nje ya mji wa Listra.

hakujiacha mwenyewe bila ya shahidi

Hii inaweza pia kuwekwa katika hali chanya. "hakika Mungu ameacha shuhuda" au "hakika Mungu ameshuhudia"

kwa kuwa

"kama inavyooneshwa na ukweli kuwa"

akiwajaza mioyo yenu kwa chakula na furaha

Hapa "mioyo yenu" inamaanisha watu. "akiwapa cha kutosha kula na vitu ambavyo vitawapa furaha"

Paulo na Barnaba wakawazuia makutano kuwatolea sadaka kwa nadra

Paulo na Barnaba waliwazuia makutano kuwatolea sadaka, lakini ilikuwa ni taabu kufanya hivyo.

wakawazuia ... kwa nadra

"walikuwa na wakati mgumu kuwazuia"

Acts 14:19

Taarifa ya Jumla:

Aliyedhaniwa kuwa amekufa ni Paulo.

kuwashawishi makutano

Inaweza kusaidia kueleza wazi alichowashawishi umati kufanya. "kuwashawishi watu kutowaamini Paulo na Barnaba, na kuwegeukia"

makundi

Hii inaweza kutokuwa kundi moja na "makutano" katika mstari uliopita. Muda umepita, na hili linaweza kuwa kundi tofauti lililokusanyika pamoja.

wakidhani kuwa amekufa

"kwa sababu walifikiri kuwa ameshakufa"

wanafunzi

Hawa walikuwa waumini wapya katika mji wa Listra.

kuingia katika mji

"Paulo aliingia tena Listra na waumini"

alienda Derbe na Barnaba

"Paulo na Barnaba walienda katika mji wa Derbe"

Acts 14:21

Taaarifa ya Jumla:

Hapa waliotangaza ijili na kuwatia mioyo wanafunzi wao inamaanisha Paulo.

Taaarifa ya Jumla:

Wanaposema "Tunapaswa" inajumuisha Paulo, Barnaba na waumini.

mji huo

"Derbe"

Waliendelea kutia nguvu nafsi za wanafunzi

Hapa "nafsi" inamaanisha wanafunzi. Hii inatia mkazo katika mawazo ya ndani na imani. "Paulo na Barnaba waliwasihi waumini kuendelea kuamini ujumbe kuhusu Yesu" au "Paulo na Barnaba waliwasihi waumini kuendelea kukua imara katika mahusiano yao na Yesu.

kuwatia mioyo kuendelea katika imani

"kuwatia mioyo waumini kuendelea kumwamini Yesu"

Acts 14:23

Taarifa ya Jumla:

Waliowachagua na kuwakabidhi kwa Bwana ni Paulo na Barnaba na walioamini ni wale walioongozwa kwa Bwana na Paulo na Barnaba.

Walipowachagua wazee katika kila kanisa

"Paulo na Barnaba walipochagua viongozi katika kila kundi jipya la waumini"

wakawakabidhi

Maana zinazowezekana ni 1) "Paulo na Barnaba wakawakabidhi wazee waliowachagua" au 2) "Paulo na Barnaba wakawakabidhi wazee na waumini wengine" (UDB)

ambaye walimwamini

Wale walioamini inategemea na chaguo lako la ni kina nani waliokuwa wanazungumziwa katika maelezo yaliyopita (mojawapo kati ya wazee au viongozi na waumini wengine).

wakaenda chini Atalia

Usemi "wakaenda chini" unatumika hapa kwa sababu Atalia iko chini kwa kimo kuliko Perge.

ambapo walikabidhiwa katika neema ya Mungu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ambapo waumini na viongozi Antiokia waliwakabidhi Paulo na Barnaba kwa neema ya Mungu" au "ambapo watu wa Antiokia waliomba kwamba Mungu awatunze na kuwalinda Paulo na Barnaba"

Acts 14:27

Taarifa ya Jumla:

Waliofika Antiokia na kutoa taarifa ni Paulo na Barnaba. Aliyefungua mlango ni Mungu.

kusanya kanisa pamoja

"wakawaita waumini wa palepale kukusanyika pamoja"

alifungua mlango wa imani kwa Mataifa

Mungu kuwawezesha Mataifa kuamini inazungumziwa kana kwambaaliwafungulia mlango uliokuwa unawazuia kuingia katika imani. "Mungu alifanye iwezekane kwa Mataifa kuamini"

Acts 15

Matendo 15 Maelezo kwa jumla

Muundo na Mpangilio

Tafsiri zingine zimeweka kila mstari wa ushairi mbele ya kulia kuliko maandishi mengine ili kurahisisha kusoma. ULB hufanya hivi na ushairi ambao umenukuliwa kutoka Agano la Kale 15:16-17

Mkutano unaoelezwa na Luka katika sura hii huitwa "Baraza la Yerusalemu." Huu ulikuwa nimuda ambapo viongozi wengi wa kanisa walikuja pamoja kuamua iwapo waumini walihitaji kufuata sheria zote za Musa.

Dhana maalum katika sura hii

Ndugu

Katika sura hii, Luka anaanza kwa kutumia neno "ndugu" kumaanisha Wakristo wenzake badala ya Wayahudi wenzake.

Kutii sheria za Musa

Waumini wengine walitaka watu wa mataifa watahiriwe kwanza kwa vile Mungu alimuambia Abarahamu kwamba yeyote aliyetaka kuwa wake lazima angepashwa tohara na hii sheria ingedumu. Kwa upande mwingine Paulo na Barnaba walikuwa wameshuhudia Mungu akiwapa watu wa Mataifa kipaji cha Roho Mtakatifu na kwa hivyo hawakusisitiza watu wa mataifa watahiriwe. Makundi yote mawili yalienda Yerusalemu kwa uamuzi wa viongozi wa kanisa kuhusu swala hilo.

"Mjiepushe na vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, na damu, na nyama zilizosongolewa, na uasherati."

Kuna uwezekano ya kwamba viongozi wa kanisa walitoa uamuzi kwa hizi sheria ili Wayahudi pamoja na watu wa Mataifa waweze kuishi pamoja na kula chakula kimoja pamoja.

<< | >>

Acts 15:1

sentensi unganishi:

Paulo na Barnaba bado wapo Antiokia wakati kulikuwa na malumbano kuhusiana na kutahiriwa kwa watu wa Mataifa

waliwafundisha ndugu

ndugu ina maana ya watu walioamini

Acts 15:3

ujumbe wa jumla

maneno yeye au wao yanamtaja Paulo

kwa kutumwa kwao na kanisa

kanisa hapa linamaanisha watu waliokuwa sehemu ya kanisa

Acts 15:5

lakini watu fulani

hapa Luka anatofautisha watu wanaoamini kuwa wokovu ni kwa Yesu pekee na wale wanaoamini kuwa wokovu ni kwa Yesu lakini pia wanaamini juu ya kutahiriwa kuwa ni muhimu kwa ajili ya wokovu

kutunza sheria ya Musa

kutii sheria ya Musa

Acts 15:7

kwa mdomo

mdomo hapa unamaanisha Petro

aliwapa wao Roho Mtakatifu

alimwacha Roho Mtakatifu aje juu yao

Acts 15:10

sentensi unganishi:

Petro anamaliza mazungumzo yake na mitume pamoja na wazee

baba zetu

hii inamaanisha wazee wa Kiyahudi

Acts 15:12

Ujumbe wa jumla:

neno wao hapa linamaanisha Paulo na Barnaba

kusanyiko lote

kila mtu, au kundi lote

Mungu alifanya

Mungu alitenda, au Mungu alisababisha

Acts 15:13

Sentensi unganishi:

Yakobo anaanza kuongea na mitume na wazee

kwa ajili ya jina lake

kwa ajili ya jina la Mungu

Acts 15:15

Sentensi unganishi:

Yakobo anamnukuu nabii Amosi kutoka Agano la Kale

kubaliana na hili

thibitisha ukweli

jina langu

hii inamaanisha Mungu

Acts 15:19

wanaomgeukia Mungu

Mtu anayeanza kumtii Mungu

kumsoma Musa

hii ina maana ya kusoma sheria za Musa

Acts 15:22

kanisa lote

hii ina maana ya watu wote waliopo kanisani

Sisilia

Hili ni jina la kisiwa katika jimbo la Asia ndogo

Acts 15:24

kuchagua wanaume

watu waliotumwa walikuwa Yuda aitwaye Barsaba na Sila

Acts 15:27

Damu

hii inamaanisha kunywa damu au kula nyama yenye damu

kwa heri

hii inamaanisha mwisho wa barua

Acts 15:30

manabii pia

manabii walikuwa ni walimu walioidhinishwa na Mungu kuongea kwa niaba yake

ndugu

walioamini wenzake

Acts 15:33

neno la Bwana

hii ina maana ya ujumbe wa Mungu

Acts 15:36

turudi sasa

nashauri turudi sasa

Pamfilia

hili ni jimbo katika Asia ndogo

Acts 15:39

na kisha akaenda

hii inamaanisha kuwa Sila alikuwa na Paulo na kisha akaondoka

alipita Siria na Sisilia

Haya ni maeneo katika Asia ndogo

Acts 16

Matendo 16 Maelezo kwa jumla

Dhana maalum katika sura hii

Kutahiriwa kwa Timotheo

Paulo alimtahiri Timotheo kwa vile walikuwa wanahubiri ujumbe wa Yesu kwa Wayahudi na watu wa Mataifa. Paulo alitaka Wayahudi wajue kwamba aliheshimu sheria za Musa ingawa viongozi wa kanisa Yerusalemu walikuwa wameamua kwamba Wakristo hawana haja ya tohara.

Mwanamke aliyekuwa na pepo wa uaguzi

Watu wengi hupenda sana kujua yanayojiri siku za usoni, lakini sheria za Musa zilisema kwamba ni dhambi kuongea na roho za wafu ili kujua yajayo. Inaonekana huyu mwanamke alijua kutabiri yajayo vyema.Alikuwa mtumwa aliyetumiwa na wenyeji wake kujitajirisha kutokana na kazi hii yake. Paulo alitaka aache kutenda dhambi, na kwa hivyo aliamuru huyo pepo amtoke. Luka hatuelezi iwapo alianza kumfuata Yesu ama hata jambo lingine kumhusu.

<< | >>

Acts 16:1

Sentensi ungsnishi

Hii sehemu ya hadithi ni kuhusu safari ya Paulo na Sila. Hapa Timotheo alitambuisha kwenye hadithi na kujiunga na Paulo na Sila. Mstari wa 1 na 2 hutoa taarifa za msingi kuhusu Timotheo

Tazama

Neno "Tazama" inatutaadharisha juu ya mtu mpya katika simulizi. Lugha yako huenda ikawa na njia ya kufanya hivyo.

Kijana aliyezaliwa na mama wa Kiyahudi ambaye ni muumini

"Kijana aliyezaliwa na mama wa Kiyahudi ambaye anamwamini Kristo.

Aliongelewa vizuri

"Timotheo alikuwa na tabia nzuri" au "Walioamini walisema mambo mazuri juu ya Timotheo"

Paulo alimtaka ili asafiri naye, hivyo akamchukua

"Paulo alimtaka Timotheo asafiri naye hivyo Paulo akamchukua" maneno mengine kama (yeye, yake) yanamrejea Timotheo.

baba yake ni Mgiriki

Kama Mgiriki, baba yake Timotheo hangeweza binafsi kumtahiri Timotheo hivyo Paul alimtahiri. Tohara mara nyingi ilifanywa na Mwalimu wa Kiyahudi, kama vile Paulo.

Acts 16:4

walipo kuwa wakienda

"Walipo kuwa" hii inamaanisha Paulo, Sila na Timotheo.

ili kuyatii

'Kwa washiriki wa kanisa kutii' au 'kwa waumini kutii'

yaliandikwa na mitume na wazee huko Yerusalemu

"ambayo imeandikwa na mitume na wazee huko Yerusalemu"

Makanisa yakaimarishwa

"Paulo , Sila na Timotheo waliimarisha makanisa"

Acts 16:6

Firigia na Galatia

Haya ni majimbo huko Asia

walikatazwa na Roho Mtakatifu

"Roho Mtakatifu aliwakataza wao" au " Roho Mtakaifu hakuwaruhusu"

Misia....Bithinia

Haya ni majimbo mengine mawili zaidi huko Asia

Roho wa Yesu

"Roho Mtakatifu"

Acts 16:9

Maono yalimtokea Paulo

Maono ni tofauti na ndoto.

akimwita yeye

"akimuomba Paulo" au "akimsihi Paulo"

mtusaidie

"Unisaidie na watu wengine wa Mekedonia"

kujiandaa kwenda

Neno "tukajiandaa" inajumuisha Paulo pamoja na wale waliokuwa naye, hii ni pamoja na Luka ambaye ndiye muandishi wa kitabu cha Matendo ya Mitume.

Mungu alituita

Alituita, hii inajumuisha Paulo pamoja na wale waliokuwa naye, hii ni pamoja na Luka ambaye ndiye muandishi wa kitabu cha Matendo ya Mitume.

Kuwahubiria injili

"kuhubiri injili kwa watu wa Makedonia"

Acts 16:11

Sentensi unganishi

Msatri wa 13, ni mwanzo wa hadithi ya Lidia. Hii ni hadithi fupi iliyotokea wakati wa kusafiri kwa Paulo

tukaenda

"tukaenda" hii inajumuisha Paulo pamoja na wale waliokuwa naye, hii ni pamoja na Luka ambaye ndiye muandishi wa kitabu cha Matendo ya Mitume.

Somathrake ...Neapoli

Hizi ni miji ya mwambao karibu na Philipi.

Utawala wa Kirumi

ni sehemu ambayo Warumi waliteka na kuishi kwa muda huo, hasa maaskari

Acts 16:14

Sentensi unganishi

Hii ndyo mwishowa hadithi ya Lidia

Mwanamke mmoja aitwaye Lidia

"Kulikuwa na Mwanamke aitwaye Lidia"

muuzaji wa zambarau

"Mfanya biashara aliyeuza nguo za zambarau"

kumuabudu Mungu

Mwenye kumuabudu Mungu ni Mataifa ambaye hutoa sifa kwa Mungu na kumfuata Yeye, lakini hafuati sheria zote za Kiyahudi.

alitusikiliza

"Yeye alitusikiliza"

mambo yaliyozungumzwa na Paulo

"Mambo ambayo paulo aliyasema "

Baada ya kubatizwa yeye na nyumba yake

"walipo mbatiza Lidia na watu wa nyumbani mwake"

Acts 16:16

Sentensi unganishi

Hii ni hadithi nyingi inayotokea wakati wa kusafiri kwa Paulo. Hii ni tukio la kwanza katika hadithi, ni habari ya mbashiri mdogo.

msichana mmoja

"kulikuwa na mwanamke mdogo"

pepo la utambuzi

roho mbaya huongea naye kuhusu habari ya maisha ya watu ya baadaye.

Alimletea bwana wake faida vyingi kwa kubashiri

hii ni habari ya nyuma kuhusu mchana huyo

akiwa amekasirishwa na yeye

"alisumbuliwa na yeye" au " alijisikia vibaya kwa kile kitu anachokifanya"

aligeuka

"Paulo aligeuka nyuma" au " alikwenda kumkabili yule msichana nyuma yake"

akatoka na kumuacha mara moja

"na pepo akatoka mara moja"

Acts 16:19

mabwana zake

wale wanao mmiliki yule msichana mtumwa

tumaini la faida

Hii inamaanisha ule uwezo wa kubashiri aliokuwa nao yule msichana na watu kumlipa kwa kuwabashiria.

kuwaburuza wao

Mabwana waliwaburuza "Paulo na Sila" lakini siyo kundi lote akiwemo Luka na Timotheo.

mbele ya wenye mamlaka

'Katika uwepo wa mamlaka' au 'kuhukumiwa na mamlaka

Walipowafikisha kwa mahakimu, walisema,

"Baada ya mabwana kuwaleta Paulo na Sila mbele ya mahakimu, mabwana wale wakasema"

Wanafundisha

"Paulo na Sila wanafundisha"

siyo ya kisheria

mabwana wanajumuisha mambo ya kitawala katika madai yao kwani wao pia walikuwa raia wa Kirumi

Acts 16:22

mahakimu wakararua nguo zao na kuwavulia

Mahakimu walirarua nguo za Paulo na Sila na kuwavulia"

na kuwaamuru wachapwe na viboka

"Kumuamuru maaskari kumchapa Paulo na Sila kwa viboko"

waliwatupa

"mahakimu waliwaweka Paulo na Sila" au " mahakimu waliwaamuru maasakari kumuweka Paulo na Sila"

na kumuamuru askari wa gereza kuwalinda vema

Askari wa gereza ni mtu anayehusika na wafu wote waliowekwa jela au gerezani. "kumuambi mlinzi wa gereza ahakikishe kuwa hawatoki nje"

kuwafunga

"kuwafungia imara katika sehemu"

nguzo

ni kipande cha mti iliyo na matobo kwa ajili ya kuwekea miguu ya mtu ili imzuiye mtu huyo asiweze kwenda.

Acts 16:25

Sentensi unganishi

Hii ni tukio lingine katika hadithi; inahusu Paulo na Sila gerezani na mlinzi wa gereza

wakiwasikiliza wao

"Neno wao" linamaanisha Paulo na Sila, ambao walikuwa wakiomba na kuimba nyimbo za kumsifu Mungu.

na misingi ya gereza ikatikiswa

"ambayo ilitikisa misingi ya gereza"

minyororo yao ikalegezwa

"minyororo yao waote ilifunguka"

Acts 16:27

ili kujiuwa

Mlinzi wa gereza alichagua kujiuwa kuliko kukabiliana na aina ya mateso yatakayo mpata kwa kuwaruhusu wafungwa kutoroka.

wote tuko mahali hapa

Neno "wote" linajumuisha Paulo, Sila na wafungwa wengine wote.

Acts 16:29

kwa haraka

"aliingi kwa haraka ndani ya gereza"

akawaangukia Paulo na Sila

"Mlinzi wa gereza alijinyenyekesha kwa kuinama mbele ya Paulo na Sila.

na kuwatoa nje

"kuwaongoza nje ya gereza"

Acts 16:32

Sentensi unganishi

wakanena, hapa inamaanisha Paulo na Sila..

nyumbani mwake

Mlinzi wa gereza aliwaleta Paulo na Sila nyumbani kwake"

yeye pamoja na watu wa nyumbani mwake wakabatizwa

"Paulo na Sila walimbatiza Mlinzi wa gereza pamoja na watu wote wa nyumbani kwake"

yeye...naye

Maneno haya yanamaanisha Mlinzi wa gereza

kwasababu wote waliamini

"kwasababu watu wote wa nyumbani kwake waliamini"

Acts 16:35

Sentensi unganishi

Hii ni tukio la mwisho kwenye hadithi. Inahusu Paulo na Sila kuwachiwa kutoka gerezani

ilipokuwa mchana

Hii ni mwanzo wa habari nyingine

walituma ujumbe

"kutuma ujumbe" au Kutuma amri"

waruhu hao wanaume

"waruhusu hao wanaume" au "waruhusu hao wanaume waende"

tokeni nje

"tokeni nje ya gereza"

Acts 16:37

akawaambia

"kusema na walinzi"

Hadharani

"mahakimu walifanya hatharani"

walitupiga , wanaume ambao

Neno "walitupiga", lina maanisha Paulo na Sila

hapana,

Paulo hapa anawajibu mahakimu au wakuu wa mji, japo anaongea na mlinzi wa gereza. " Haitawezekana"

Warumi

Hii ina maana ya wananchi wa kisheria ya Dola. Uraia zunatoa uhuru wa kutoteswa na haki katika kesii. Viongozi wa mji walikuwa na hofu kuwa inaweza kufahamu jinsi viongozi wa jiji walivyo wanyanyasa Paulo na Sila.

wao wenyewe waje

"watawala wa mji waje"

Mahakimu wakaja na kuwasihi

"mahakimu walikuja na kumsihi Paulo na Sila"

baada ya kuwatoa

"baada ya mahakimu kuwaondoa Paulo na Sila"

Acts 16:40

Sentensi unganishi

"Hii ni mwisho wa hadithi ya Paulo na Sila kuwa gerezani"

Taarifa za ujumla

Fungu hili linazungumzia habari a Paulo na Sila pamoja na Waumini wa mji wa Philipi.

Nyumba ya Lidia

"nyumbani kwa Lidia"

walipowaona ndugu

Neno "ndugu" linamaanisha waumini wa jinsi zote. Waliwaona waumini.

Acts 17

Matendo 17 Maelezo kwa jumla

Dhana Maalum katika sura hii

Kutoelewana kuhusu Maasiya

Wayahudi walimtarajia Kristo ama Maasiya awe mfalme mwenye nguvu kwa vile Agano la Kale limesema hivyo mara nyingi. Agano hilo pia lizungumzia wakati ambapo Maasiya angeteseka na hayo ndio Paulo alikuwa akiwaambia Wayahudi. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#christ)

Dini ya Athene

Paulo alisema kwamba watu wa Athene walikuwa watu wa "Kidini" lakini hawakumuabudu Yahweh. Waliiabudu miungu wengi wasio kweli. Hapo awali waliwaleta watu wengi chini ya utawala wao na baadaye wakaanza kuabudu miungu zao. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#falsegod)

Katika sura hii Luka anafafanua kwa mara ya kwanza jinsi Paulo alivyo waambia ujumbe wa Kristo kwa wale hawakufahamu lololete kuhusiana na agano la kale.

<< | >>

Acts 17:1

Sentensi unganishi

Habari kuhusu Paulo na Sila inaendelea pamoja na Timotheo katika safari yao ya kimisionari. Walifika Thesalonike na Luka hakuwa pamoja nao.

Taarifa za jumla

Ni habari kuhusu Paulo na Sila pamoja na Wayahudi katika Sinagogi huko Thesolanike

Sasa

Ni neno linalogawanya habari iliyokuwa ikiendelea kwa kutaja jambo jingine. Luka anaanza kuelezea sehemu mpya ya tukio.

walipopita

"Kusafiri kupitia"

miji ya Amfipoli na Apolonia

Hii ni miji ya mwambao huko Makedonia

walifika mjini

Neno linaloonyesha kuwa walisafiri hadi kufika mjini.

kama ilivyokuwa kawaida

" kama ilivyokuwa kawaida yake" au "Kama alivyofanya siku zote". Mara kwa mara Paulo alikuwa na ya kuingia kwenye Sinagogi siku ya sabato mahali wayahudi walikusanyuka.

kwa sabato tatu

"katika kila siku ya sabato kwa majuma matatu".

alihojiana nao kutoka kwenye maandiko

"alijadiliana na Wayahudi wa Sinagogi" au walijadili na Wayahudi wa Sinagogi"

alihojiana nao

"aliwapa sababu" au "kuhojiana pamoja nao" au "kuzungumza pamoja nao".

Acts 17:3

Alikuwa akifungulia maandiko

Maana inawezekana ni 1) "Paulo alikuwa akieleza maandiko kwa usahihi ili watu waweze kuwa na uwezo wa kuelewa ni nini alikuwa akifundisha" au 2) "Paulo alikuwa akifungua kitabu au kitabu cha maandiko."

ilimpasa

"ilikuwa ni sehemu ya mipango ya Mungu"

kufufuka tena

"kurudi tena katika uhai"

kutoka wa wafu

"kutoka miongoni mwa wafu" anaelezea juu ya roho za watu ambao wamekwisha kufa. Kurudi kutoka miongoni mwao kunamaanisha kurudi katika uzima tena.

Wayahudi walishawishika

"Wayahudi walishawishika " au "Wayahudi walikubali"

na kuungana na Paulo

"na kuwa na ushirika na Paulo"

Wagiriki wacha Mungu

wale wenye kumcha Mungu lakini hawajabadilishwa kuingia dini ya kiyahudi kwa njia ya kutahiriwa.

umati mkubwa

"ni umati mkubwa wa watu"

Acts 17:5

Maelezo ya jumla

Fungu hili linajadili juu ya Wayahudi wasioamini na wanaume wengine waovu kutoka sokoni.

waliojawa na wivu

"Ni hali ya wivu inayoleta msukumo ndani ya mtu" "Kuwa na wivu sana" au "Kuwa na hasira sana"

kwa wivu

Inaelezwa kuwa hawa Wayahudi walikuwa na wivu kwasababu baadhi ya Wayahudi wa Kiyunani wakiuamini ujumbe wa Paulo.

kundi maalumu la wanaume waovu

"baadhi ya wanaume waovu"

kutoka eneo la sokoni

"Kutoka eneo la wazi la mkusanyiko" Ni eneo la wazi la kufanyia biashara ya kuuza na kununua bidhaa, Ng'ombe au eneo la kutolea huduma.

kuusimamisha mji kwa ghasia

Mji kusimamisha kazi zake kutokana na ghasia.

wakaivamia nyumba

"Kuingia kwa vurugu na kuivamia nyumba kwa nguvu" . Hii inawezekana walikuwa wakiirushia mawe nyumba na kutaka kuvunya mlango wa nyumba.

Jason

Hili ni jina la mtu.

kuwaleta mbele za watu

"Kundi la watu Serikalini au kundi la watu raia wa nchi walikusanyika ili kufanya maamuzi"

mbele ya maofisa

"mbele ya Viongozi"

Hawa wanaume walio

Viongozi wa Kiyahudi waliongea wakimaanisha Paulo na Sila kwa kusema "Hawa wanaume"

walioupindua ulimwengu

Hiki Kifungu inawakilisha namna nyingin ya Kusema Paulo na Sila wanasabisha ghasia. Viongozi wa Kiyahudi wanatia chumvi juu ya ushawishi walionao Paulo na Sila katika mafundisho yao.

waliokaribishwa na Yasoni

Hii kifungu inaashiria kuwa Yasoni alikubaliana na mitume waliokuwa wakieneza ujumbe wa machafuko

Acts 17:8

Taarifa za jumla

Fungu hili linazungumzia wale waheshimiwa wa mji huo.

waliingiwa na wasiwasi

"kufadhaika" au "kuwa na mashaka kiakili"

walikuwa wamaukua fedha ya ulinzi kutoka kwa Jason na baadhi ya watu wengine.

Fedha hii ilikuwa ahadi ya mwenendo mzuri, ambayo inaweza kurudishwa kama mambo yote yataenda vizuri, au kutumika kukarabati uharibifu uliosababishwa na mwenendo mbaya. "walipokea dhamana" au "amana" au "faini"

na wengine

"waumii wengine mbali na Yasoni"

Acts 17:10

Taarifa ya Jumla

Hii ni sehemu nyingine ya habari kuhusu Paulo na Sila safarini. Kwa sasa wako Beroya"

ndugu

Neno "ndugu" linamaanisha wanaume na wanawake walioamini"

Hawa watu walikuwa waungwana mno

Ni watu waliokuwa na utayari wa kufikiri kwa hali ya kupokea mawazo mapya zaidi ya watu wengine'.

walipokea neno

"kusikiliza mafundisho"

kwa utayari wa akili zao

"Hao Waberoya walikuwa wamejiandaa kuchunguza mafundisho ya Paulo kulingana na maandiko"

kuchunguza maandiko kila siku

"kusoma kwa umakini na kupima uhalisia wa kifungu cha maandiko kila siku"

mambo haya yaliendelea hivyo.

"Maneno aliyoyasema Paulo yalikuwa ya kweli.

Acts 17:13

Taarifa ya jumla

Athene ni mji uliokuwa chini ya pwani kutoka Beroya ambayo ni Makedonia. Atheni ulikuwa moja ya miji muhimu zaidi katika Uyunani.

walipogundua

"walipoambiwa" au "walipojulishwa" au "waliposikia"

walikwenda huko na kuchochea

Hii inazungumzia kuhusu watu walioshawishwa kama mtu anayechanganya kemikali ili kutoa mlipuko. Waliwaendea na kuwashawishi kutenda isivyo.

kuanzisha ghasia katika umati

"kusababisha hofu na wasiwasi miongoni mwa watu"

Ndugu

Neno "ndugu" linamaanisha wanaume na wanawake walioamini"

waliompeleka Paulo

"Walioambatana na Paulo" au "waliokwenda pamoja na Paulo"

Walipokea kwake maelekezo kuhusu Silas na Timotheo.

"Aliwaambia wawaelekeze Silas na Timotheo"

Acts 17:16

Taarifa ya jumla

Hii ni sehemu nyingine ya hadithi ya Paulo na Sila wakiwa safarini. Paulo kwa sasa yuko Athene akiwangojea Silas na Timotheo kuungana naye.

roho yake iikasirishwa kuona mji umejaa na miungu ya sanamu.

"alisumbuliwa" au "alifadhaika" au "akawa na huzuni"

akajadiliana

Hili neno linaashiria kuwa kulikuwa na majibizano zaidi kutoka kwa wasikilizaji kuliko katika kuhubiri. "alijadiliana"

sokoni

Hii ni sehemu ambayo watu huuza na kununua vitu, ngombe, au huduma hutolewa. " sehemu ya umma"

Wale waliokuwa wakimwabudu Mungu

Inamaanisha Watu wa mataifa waliokuwa wakimsifu Mungu na kumfuata ingawa hawakuwa wakifuata taratibu za ibada ya Kiyahudi.

Acts 17:18

Waepikureo na Wastoiko.

Watu hawa waliamini mambo yote yalifanywa kwa bahati na kwamba miungu walikuwa na shughli zao na walifurahi kutobuguziwa katika kuiongoza ulimwengu. Walikataa ufufuo na walitaka maisha rahisi ya raha pekee.

Wanafalsafa wa Wastoiko

Watu hawa waliamini uhuru unatokana na kujiwekea mwenyewe hatima yako. Walikataa Mungu anayependa binafsi na ufufuo.

wakamkabili yeye

"walimkabii Paulo"

na baadhi wakasema

"na baadhi ya wanafilosofia wakasema"

Ni nini huyu msengeaji

'Babbler' ilitumika kwa kutaja ndege kuokota mbegu kama chakula. Ilihusu ubaya wa wasengenyaji. Wanafalsafa walisema Paulo alikuwa na baadhi ya habari ambazo hazikuwa na thamani ya kusikiliza

wengine wakasema

"Wanafilosopha wengine wakasema"

Inaonekana ni muhubiri

"Inaonekana ni mtu ayetangaza " au "anaonekana yuko katika umisheni wa kusambaza habari'

Acts 17:19

Wakamchukua

Wanafalsafa wa Waepikureo na Wastoike walimchukua Paulo"

na kumleta Areopago

kilima katika Athene juu ambayo mahakama kuu ya Waethene ambapo huenda walikutana.

Twaweza kujua haya mafundisho mapya unayoyaongea

"Twaweza" hapa inamaanisha mafilosopha peke yao. "'Tunataka kufanya uamuzi juu ya mambo haya unayodai "

wote wa Athene

"Wananchi wa Athene" ni watu kutoka Athene, mji karibu na pwani katika Makedonia (sasa ni Ugiriki)

na wageni

"Mtu mgeni" au "mtu mpya katika jamii ya Athene"

hutumia muda wao kwaq hasara

"walitumia muda wao "au "hutumia muda wao"

kuongea na kusikiliza juu ya jambo jipya

"Kujadili mawazo mapya ya falsafa" au "kuzungumza juu jambo jipya kwao'

Acts 17:22

Taarifa ya Jumla

Paulo alianza mahubiri yake kwa wanafilosofia wa Areopago.

weny dini hasa katika kila namna

Paulo alikuwa akirejea jinsi Waathene wanavyoonyesha hadharani kuheshimu miungu kwa sala, kujenga madhabahu na kutoa dhabihu

kwani nilipokuwa nikipita

"kwasababu nilipotembea na kupita"

KWA MUNGU ASIYEJULIKANA

Inaweza ikawa na maana zifuatazo 1) "mungu fulani asiyejulikana" au 2)"kwa mungu yeyote tusiyemjua

Acts 17:24

Dunia

Kwa hali ya ujumla "dunia" inamaanisha mbingu na ardhi na kila kitu kilichoko ndani yake.

kuwa Yeye ni Bwana

"Yeye" inarejea yule Mungu asiyefahamika ambaye Paulo anawaelezea kuwa ni Bwana Mungu. "kwasababu ni Mungu"

yaliyojengwa na mikono

"kupitia matendo ya watu"

hatumikiwi na mikono ya wanadamu

"Kutumikiwa" ni ile hali ambayo Daktari anapomhudumia mgonjwa ili apone. "kujali kwa"

Kwa mikono ya watu

"kwa mikono ya wanadamu"

Kwani Yeye

"kwasababu Yeye mwenyewe"

Acts 17:26

mtu mmoja

Inaweza kuwa na maana zifuatazo .1) "ni Adamu ambaye Mungu alimuumba" au 2) "Inaweza ikajumuisha Adamu na Hawa ambao Mungu aliwaumba"

alifanya Mataifa

"Mungu,muumbaji, alifanya mataifa yote"

yote ...wao

Hapa inamanisha watu wote waishio juu ya uso wa dunia.

kwahiyo

neno hili ni alama ya kauli kwamba alisema kwasababu ya kile ambacho alisema hapo awali.

kumtafuta Mungu japo hayuko mbali nao

"Kumtafuta Mungu"

wamfikie

"kuona haja ya Yeye"

hayuko mbali

Paulo anasema kinyume ya kile anachozungumza ili kusisitiza jambo. " Yeye yuko karibu sana"

na kila mmoja wetu

Paulo anajiweka mwenyewe, wasikilizaji wake na kila taifa alipotumia neno "kila mmoja wetu"

Acts 17:28

Kwake

"Kwa Mungu"

Tunaishi na Kutembea

Paulo anajumuisha wasikilizaji wake na yeye mwenyewe.

tu wazaliwa wake

Hapa 'tu wazaliwa wake' ni wazaliwa ambao wanaweza kuwa si watoto wa sasa. Wao kushiriki baadhi ya sifa pamoja na babu zao. 'Wake' ni kiwakilishi kisichojulikana katika nukuu hii.

kuwa uungu

Hapa "uungu" inarejea hali ya Mungu au sifa zake.

Acts 17:30

Taarifa unganishi

Paulo alimaliza mazungumzo yake na wanafilosofia wa Areopago, aliyokuwa ameianza.

Kwahiyo

neno hili ni alama ya kauli kwamba alisema kwasababu ya kile ambacho alisema hapo awali

Mungu hakuzijari nyakati za ujinga

Inaweza kuwa na maana zifuatazo 1) "kwamba hawajui kuhusu kitu chochote" au 2) " kumkataa kwa makusudi"

Wakati atakapo wahukumu walimwengu kwa haki kwa njia ya mtu aliyemchagua

hapa, neno "walimwengu" inarejea watu waishio duniani.

kwa mtu ambaye alimchagua

"kwa mtu ambaye Mungu alimchagua"

Mungu alitoa uhakika wa mtu huyu

"Mungu alionyesha uchaguzi Wake kwa mtu huyu"

Acts 17:32

Taarifa unganishi

Hii ni sehemu ya mwisho wa hadithi kuhusu Paulo akiwa huko Athene

na watu wa Athene

Wale watu waliokuwepo pale Areopago wakimsikiliza Paulo

baadhi yao wakamdhihaki Paulo

Wale hawakuamini kuwa inawezekana kwa mtu yeyote kufa na kurudi tena kwenye maisha. "Baadhi walimdharau" au "baadhi walimcheka Paulo"

Sisi tutakusikiliza

"sisi" inarejea watu wa Athene ambao walitaka kumsikiliza Paulo. Waliongea moja kwa moja kwa Paulo lakini si pamoja Paul katika kundi lao."

Dionisio Mwareopago, na Mwanamke anaitwa Damari

Dionysius ni jina la mtu. Areopago ina maana kwamba Dionysius alikuwa mmoja wa majaji katika Areopago.

Acts 18

Matendo 18 Maelezo kwa ujumla

Dhana maalum katika sura hii

Ubatizo wa Yohana

Wayahudi wengine walioishi mbali kutoka Yerusalemu na Judea walisikia kumhusu Yohane Mbatizaji na wakafuata mafundisho yake. Walikuwa bado kusikia habari za Yesu. Mmoja wa hao aliitwa Apollo. Alimfuata Yohane Mbatizaji lakini hakufahamu kwamba Maasiya alikuwa aliisha kuja. Yohane aliwabatiza watu kuonyesha ya kwamba walitubu dhambi zao na lakini ubatizo huu ulikuwa tofauti na ubatizo wa Kikristo. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faithful and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#christ and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#repent)

<< | >>

Acts 18:1

Taarifa ya jumla

Hii ni sehemu nyingine ya hadithi ya safari ya Paulo. Kwa sasa yuko Corintho. Akwila na Priskila wanatambulishwa kwenye hadithi katika mstari 2 na 3 inatoa habari ya nyuma kuhusu wao.

baada ya mambo hayo,

"baada ya matukio hayo kufanyika huko Athene"

Huko akampata

Inaweza kuwa na maana kwamba: 1) "Paulo alitokea kumpata kwa bahati" au 2) "Paulo alimpata baada ya kuwatafuta kwa nia.'

Mtu mmoja aliyeitwa Akwira

Hapa anamtaja mtu yule aliyemwona huko naye ni Akwira.

mzaliwa wa Ponto

Ponto ilikuwa mkoa katika pwani ya kusini ya Bahari ya Nyeusi.

alikuwa amehamia karibuni

"Hii huenda ni muda fulani kwa miaka ya nyuma"

Italia

Jina hili ni la nchi. Roma ni mji mkuu wa Italia.

Klaudia alikuwa ameagiza

Klaudia alikuwa ndiye Kaisari wa Kiroma kwa sasa.

Alikuwa akifanya biashara waliyoifanya

Alikuwa akifanya aina ya kazi waliyoifaya na wao.

Acts 18:4

Taarifa ya jumla

Sila na Timotheo walioungana na Paulo

Kwahiyo Paulo akajadiliana

Hapa "kujadiliana" inamaanisha Paulo alikuwa na maongezi ya pande mbili". "kwa hiyo walijadiliana"

Aliwashawishi

"aliendelea kujaribu kuwashawishi"

Paulo alisukumwa na Roho

Paulo alizidi kusukumwa na Roho.

akakung'uta vazi lake

Hii ni hatua ya mfano zinaonyesha kwamba Paulo alikata mahusiano na Wayahudi wasioamini na kuwaacha kwa hukumu ya Mungu.

Damu yenu na iwe juu ya vichwa vyenu wenyewe

Hapa "damu" inalinganishwa na adhabu ya dhambi. Paulo anawaambia Wayahudi hao kuwa watawajibika kwa ajili ya hukumu watakayokabiliana nao kwa sababu ya ukaidi wa kukataa kutubu. "Ninyi peke yenu mtabeba jukumu la adhabu yenu kwa ajili ya dhambi zenu".

Acts 18:7

Kauli ya jumla

maelezo ya fungu hili yanazungumzia habari za Tito Yusta na Krispas

Tito Yusto...Krispo

Ni majina ya wanaume

alimwabudu Mungu

Ni mwabudu Mungu wa kimataifa ambaye alimtukuza Mungu na kumfuata, lakini si kwa njia ya kushika sheria za Kiyahudi.

Kiongozi wa sinagogi

ni mtu wa kawaida ambaye hufadhili na kuhudumia sinagogi, na si lazima awe mwalimu.

na watu wa nyumbani mwake

"watu walioishi na yeye ikiwa ni pamoja na ndugu na jamaa zake"

Watu wengi wa Korintho walibatizwa

"Watu wengi wa Korintho ambao siyo Wayahudi" walibatizwa

Acts 18:9

usiogope, lakini ongea na usinyamaze

Bwana anatoa amri moja katika njia mbili tofauti -"usiwe na hofu" na "Sema na wala usinyamaze"'-kufanya maneno yake kuwa na nguvu. "N lazima kuacha kuwa na hofu, na badala yake endelea kusema na usikae kimya.'

Ongea na usinyamaze

Mungu anamuamuru Paulo kwa nguvu aongee. " Hakika ni lazima uongee"

usinyamaze

"usinyamaze kuongelea kuhusu injili"

kwani Mimi niko pamoja nawe

"Mimi" inamaanisha Bwana, ambaye anaongea na Paulo.

Niko nawe

"nawe" inamaanisha Paulo , ambaye Bwana anaongea naye kwa njia ya maono.

nina watu wengi katika mji huu

"Kuna watu wengi katika mji huu walioweka imani yao kwangu"

Paulo akakaa huko...,akifundisha neno la Mungu miongoni mwao.

Hii ni kauli ya kumalizia kwa sehemu hii ya hadithi.

Acts 18:12

Taarifa ya jumla

Hili ni tukio jipya katika hadithi. Paulo aliletwa kwenye kiti cha hukumu mbele ya Galio.

Galio alipofanywa mtawala wa Akaya

Akaya ilikuwa jimbo la Roma ambao Korintho ilikuwa sehemu yake ambayo sasa inafahamika kama kusini mwa Ugiriki.

kumleta yeye mbele ya kiti cha hukumu

Wayahudi walimshika Paulo kwa nguvu na kumleta Paulo mbele ya mahakama. "walimpeleka ili akahukumiwe na mtawala"

Acts 18:14

Galio akasema

Galio alikuwa gavana wa Kirumi wa Mkoa.

sheria zenu

Hayo yalikuwa ni sheria ya Musa na desturi nyingine za kiyahudi wakati wa Paulo

Mimi sitamani kuwa hakimu kwa habari ya mambo hayo

Mimi nakataa kufanya hukumu kuhusiana na mambo hayo"

Acts 18:16

Taarifa za jumla

Fungu linaelezea watu wamataifa mbele ya baraza. Waliitikia kinyume cha wayahudi waliokuwa wamemleta Paulo mbele ya kiti cha hukumu.

Galio aliwafanya wote waondoke mbele ya kiti cha hukumu

Galio aliwaaga waondoke mbele yake na kiti chake cha hukumu.

wote wakamkamata

Hali hii ya kutia chumvi ni kusisitiza hisia kali watu waliyokuwa nayo . "watu wengi walimkamata" au "wengi wao walimshika"

Hivyo walimkamata Sosthene, kiongozi wa sinagogi, na kumpiga mbele ya kiti cha hukumu.

Inamaanisha 1)"Watu wa Mataifa walimpiga Sosthene mbele ya kiti cha hukumu kwasababu alikuwa kiongozi wa Kiyahudi. Au 2) Sosthene alikuwa Myahudi Mkristo hivyo wayahudi walipandwa na hasira juu ya imani yake na kumwadhibu mbele ya kiti cha hukumu.

wakampiga

Sosthene ilipigwa mwili wake ."kupigwa" au "kuumizwa".

Acts 18:18

Sentensi Unganishi

Huu ni mwendelezo wa safari ya kimisionari ya Paulo, pamoja na Priskila na Akwila waliondoka Korintho.

Taarifa ya jumla

Kenkrea ulikuwa ni bandari katika sehemu ya mji mkuu wa Korintho.

Ndugu

Neno "ndugu" linamaanisha wanaume na wanawake walioamini

kwenda Syria kwa meli pamoja na Priskila na Akila

Paulo alipanda kwenye meli iliyokuwa inaenda Syria . Priskila na Akwila walienda pamoja naye.

Alikuwa amenyoa kichwa chake

Hii ni alama ya mfano wa tendo lililodhihirisha nadhiri kamilifu.

kujadiliana na

" kujadiliana pamoja" au "kujadiliana"

Acts 18:20

Taarifa ya jumla

Hapa wanatambulishwa Wayahudi waliokuwa wakiishi mji wa Efeso

Kuwaaga na kuondoka

"kuwaambia kwaherini"

Acts 18:22

Sentensi unganishi

Paulo anaendelea na safari yake ya kimisionari.

Taarifa ya jumla.

Frigia ulikuwa ni jimbo katika Adsia ambao kwa sasa ni Uturuki.

alipotua Kaisaria

"alifika Kaisaria kwa njia ya Meli"

alipanda kwenda

"Paulo alisafiri kwenda mji wa Yerusalemu" Kupanda kwenda juu kwa vile Yerusalimu ulikuwa nyanda za juu zaidi ya Kaisaria.

Kusalimia Kanisa la Yerusalemu

"kuwasalimia washirika wa kanisa laYerusalemu"

Akashuka kwenda

Alishuka kwenda Antiokia kwa vile Antiokia ulikuwa mji uliochini ya bonde zaidi ya Yerusalemu.

Paulo aliondoka

"Paulo alikwenda zake" au "Paulo aliondoka"

Baada ya kukaa pamoja nao kwa muda fulani.

Unazungumziwa muda alioutumia kukaa nao kabla mtu hajaanza safari nyingine.

Acts 18:24

Sentensi unganishi

Luka anaelezea kile kilichotokea katika Mji wa Efeso wakiwa na Prisila na Akwira

Taarifa ya Jumla

Apolo anatambulishwa kwenye hadithi. Mistari ya 24 na 25 inatoa habari kumuhusu yeye.

Mmoja wa Wayahudi aitwaye Apolo

Hapa Luka anaanza kuelezea habari ya mtu mpya.

Mzaliwa wa Alexandra

"Mtu ambaye alizaliwa katika mji wa Alexandria". Hii inaweza kuwa ni miji ya 1) "Alexandria huko Misiri katika mwambao wa kaskasini. " au 2) Alexandra huko Asia katika mwambao wa magharibi."

ufasaha katika kuongea

"mwongeaji mzuri"

mwenye uwezo katika maandiko

"Alikuwa anayafahamu vema maandiko. Alikuwa anauelewa mzuri wa maandiko ya Agano la Kale.

Apolo alikuwa ameelimishwa vema katika mafundisho ya Bwana.

"Baadhi ya waumini walikuwa wamemfundisha Apolo namna Bwana Yesu alivyokuwa anataka watu wapate kuishi.

Alikuwa na bidii katika roho

Neno "roho" linamtambulisha Apolo kama mtu aliyekuwa mwenye nia thabiti ya roho.

ubatizo wa Yohana

"Ubatizo ambao Yohana alifanya" Huu ni ulinganisho wa ubatizo wa Yohana ambao ulikuwa wa maji na ubatizo wa Yesu ambao ulikuwa wa Roho Mtakatifu.

njia za Mungu

Namna vile anawataka watu waishi.

kwa usahihi

"kwa undani zaidi "

Acts 18:27

Taarifa ya jumla

Akaya lilikuwa jimbo katika sehemu ya Kusini mwa Ugiriki kwa sasa

Kupitia katika Akaya

"Kwenda kupitia katika Mkoa wa Akaya"

Ndugu

Neno "ndugu" hapa linamaanisha wanaume na wanawake walioamini.

kawaandikia wanafunzi

"kuandka barua kwa Wakiristo walioko Akaya"

Wale walioamini kwa neema

"Wale waliokuwa wameamini wokovu wa Yesu wa neema"

Appolo aliwashinda Wayahudi hadharani

Appolo aliwashinda Wayahudi mbele ya watu wengine kwa hoja zake.

Kwa uwezo na ujuzi wake

"Kwa nguvu ya ushindani wa hoja zake na ujuzi wake wa kuongea"

Acts 19

Matendo 19 Maelezo kwa ujumla

Dhana maalum katika sura hii

Ubatizo

Yohane aliwabatiza watu kuwashiria kwamba walikuwa wanatubu dhambi zao. Wafuasi wa Yesu waliwabatiza watu waliotaka kumfuata Yesu.

Hekalu la Diana

Hekalu la Diana lilikuwa na umuhimu kubwa katika jiji la Efeso. Watu wengi walienda Efeso kuliona hili hekalu, na wakanunua sanamu za Diana, mungu we kike, wakati walipokuwa pale. Watu waliouza sanamu hizi za Diana walihofia kwamba watu wasingeamini kwamba Diana ni mungu wa ukweli, wangeacha kununua sanamu kutoka kwa wauzaji.

<< | >>

Acts 19:1

Sentensi unganishi

Paulo anasafiri kwenda Efeso

Taarifa ya jumla

"Nyanda za juu za nchi" lilikuwa ni eneo la Asia ambalo kwa sasa ni Uturuki kaskazini ya Efeso. Paulo alilazimika kusafiri kwa nchi kavu kuzunguka pembezoni mwa bahari ili kuweza kufika Efeso ambao pia ni Uturuki ya sasa.

Ikawa kwamba

Huu ni mwanzo wa habari mpya.

Kupita katikati

"Kusafiri kupitia"

kumpokea Roho Mtakatifu

Hii inamaanisha kuwa na Roho Mtakatifu aliyekuja juu yao.

Hatukuwahi hata kusikia kuhusu Roho Mtakatifu

Sisi hatukusikia kuhusu Roho Mtakatifu

Acts 19:3

Taarifa ya jumla

Paulo anaendeleza mjadala wake pamoja na waumini wapya huko Efeso.

mlibatizwa katika nini?

"Ubatizo wa aina gani mliobatizwa?"

Katika Ubatizo wa Yohana

"Tuliupokea ubatizo kupitia mafundisho aliyokuwa akifundisha Yohana"

Ubatizo wa toba

"Ubatizo ambao watu waliuomba wakati walipotaka kugeuka kutaka kutubu dhambi zao

yule ambaye angekuja

Hapa neno "Yule" linamaanisha Yesu.

kuja baada yake

Hii inamaanisha angekuja baada ya Yohana Mbatizaji.

Acts 19:5

Sentensi unganishi

Paulo anaendelea kuishi huko Efeso

Wakati watu

"Watu" hapa inahusu waumini wa Efeso wakizungumza na Paulo.

Wakabatizwa

Wakapokea ubatizo

Kwa jina la Bwana Yesu

Hapa "Jina" linamaanisha nguvu na mamlaka ya Yesu.

akaweka mikono yake

Akaweka mikono yake juu ya vichwa vyao wakati akiomba'

walinena kwa lugha nyingine, na kutabiri

hakuna maelezo ya ambao wanaweza kuelewa ujumbe wao

Katika yote walikuwa watu wapatao kumi na wawili

Hii ni taarifa za msingi kuhusu wanaume ambao walikuwa wamebatizwa

Acts 19:8

Paulo alikwenda katika sinagogi akasema kwa ushujaa kwa muda wa miezi mitatu

Paul mara kwa mara alihudhuria mikutano katika sinagogi kwa miezi mitatu na kusema nao kwa ujasiri

kuwavuta watu

kujaribu kuwashawishi watu kwa ujumbe wa kweli.

kuhusiana na ufalme wa Mungu

Hapa neno "Ufalme" linasimamia uongozi wa Mungu kama Mfalme.

Baadhi ya Wayahudi wengine walikuwa wagumu

Baadhi ya Wayahudi wakaidi walikataa kukubali ujumbe

Kuongea mabaya

Kuongea mambo mabaya

njia ya kristo

wokovu kupitia Yesu Kristo

katika ukumbi wa Tirano

Katika ukumbi mkubwa mahali Tirano alipokuwa akifundishia watu.

Tirano

Hili ni jina la mtu mwanaume

wote waliokuwa wanaishi Asia walisikia

Inaweza kuwa na maana ya 1) 'Paul alishirikisha injili kwa watu wengi katika Asia' au 2) 'Ujumbe wa Paulo uliwafikia wote wa Asia kutoka Efeso kutoka hadi Asia yote.

Neno la Bwana

Hapa "neno" linasimama kwa ujumbe. Ujumbe kuhusu Bwana Yesu.

Acts 19:11

Taarifa ya jumla

Fungu hili linazungumzia juu ya wale waliokuwa wagonjwa.

Mungu alikuwa akitenda makuu kupitia mikono ya Paulo hata waliokuwa wagonjwa waliponywa

Hapa "mikono" linasimamia maisha yote ya Paulo. Mungu alikuwa akimtumia Paulo kutenda miujiza.

walichukua leso na eproni kutoka mwili wa Paulo

Hivi vilikuwa vitambaa ambavyo Paulo alivivaa ama kuvitumia. Walipovigusa vitambaa amabvyo Paulo alivivaa wakati wa huduma.

Acts 19:13

Taarifa ya jumla

Huu ni mwanzo wa tukio jingine lililotokea wakati Paulo akiwa Efeso. Ni kuhusu wapunga mapepo Wayahudi.

Wapunga mapepo

watu ambao hufukuza roho wabaya kutoka kwa watu au maeneo

akilitumia jina la Yesu kwa matumizi yao wenyewe

Ingawa hawakuwa wakimwamini Yesu, walijaribu kutumia jina lake kama moja ya maneno yao ya muujiza

Walinena juu yao walikuwa wapegawa na roho chafu

Walilitaja jina la Yesu kwa roho wachafu zilizokuwa zimewapaa watu

wale waliokuwa na pepo wabaya

wale waliokuwa wakiongozwa na roho wabaya

Kwa Yesu anayehubiriwa na Paulo

"Yesu" lilikuwa ni jina la kawaida wakati ule, hivyo hao wapunga mapepo waliwataka wato kujua waliyekuwa wakimnena.

kwa Yesu

Hii inasimamia nguvu na mamlaka ya Yesu.

Waliofanya vile walikuwa wana saba wa kuhani wa kiyahudi, Skewa.

Hii ni habari inayojadili habari ya wapunga mapepo.

Skewa

Hili ni jina la mtu mwanaume.

Acts 19:15

Yesu namjua na Paulo namjua

"Namjua Yesu na Paulo" au "Nimesikia kuhusu Yesu na Paulo"

lakini ninyi ni nani?

roho aliuliza swali hili kuwathibitishia wapunga mapepo kuwa wao hawakuwa na mamlaka juu ya roho wachafu.

roho mchafu aliyekuwa ndani ya yule mtu akawarukia.

Hii inamaanisha roho mchafu alimsababisha yule mtu aliyekuwa akiongozwa naye kuwarukia hao wapunga mapepo.

Wapunga pepo

Linaelezea juu ya watu waliokuwa wakitoa roho chafu kutoka kwa watu au eneo fulani.

nao walikimbia .............. uchi

Wapunga mapepo walikimbia na kuacha nguo zao. walikimbia uchi.

Jina la Bwana Yesu liliheshimiwa

Waliliheshimu jina la Yesu ama walilifikiria jina la Bwana Yesu kuwa kuu.

Jina

Hili linasimama kwa nguvu na mamlaka ya Yesu.

Acts 19:18

Sentensi unganishi

Huu ni mwisho wa sehemu ya habari inayowahusu Wayahudi wapunga mapepo.

Wakakusanya vitabu vyao

'Walikusanya vitabu vyao'. Neno "vitabu" linaelezea aina ya magombo yaliyokuwa yakitumika kuendeshea manuizio ya uchawi kutokana na mwelekezo wa maneno yaliyoandikwa humo.

mbele ya macho ya kila mtu

mbele ya kila mtu

thamani yake

"thamani ya vitabu" au "thamani ya yale magombo"

Elfu hamsini

50,000.00

vipande vya fedha

"Kipande cha fedha" ilikuwa takriban mshahara wa siku kwa mfanyakazi wa kawaida

Hivyo Neno la Bwana likaenea kwa upana sana katika njia yenye nguvu

"Kwasababu ya matendo makuu haya, watu wengi zaidi waliusikia ujumbe kuhusu Bwana Yesu."

Acts 19:21

Sentensi unganishi

Paulo anazungumzia kuhusu uamuzi wake wa kwenda Yerusalemu, lakini hajaondoka Efeso bado

Paul anakamilisha huduma katika Efeso.

Paul anakamilisha kazi ambayo Mungu alikuwa amemwagiza kuifanya katika Efeso.

Aliamua katika roho

Inawezekana kuwa na maana ya 1) Paulo aliamua kwa msaada wa Roho Mtakatifu au 2) Paulo alikusudia kutokana na uamzi wa roho yake, ambayo inamaana alifanya uamzi wake.

Akaya

Akaya ilikuwa Jimbo la Rumi mahali ambapo Korintho ilipokuwa. Ulikuwa ni mji kubwa kusini mwa Ugiriki na mji mkuu wa jimbo.

Mimi lazima pia nikaone Rumi

Mimi lazima pia kusafiri kwenda Rumi

Lakini naye akabaki kwa muda huko Asia

Ni kufanywa wazi kwa mistari michache inayofuatia kwamba Paulo alikuwa alibakia Efeso

Acts 19:23

Sentensi unganishi

Luka anaelezea juu ya ghasia ambayo ilizuka wakati Paulo akiwa Efeso.

Taarifa ya jumla

Demetrio ametambulishwa kweny habari hii. Mstari wa 24 umeelezea kumhusu Demetrio

Taarifa ya jumla

Efeso kulikuwa na hekalu kubwa lililojengwa kwa ajili ya mungu mke Diana, Wakati mwingine imetafasiriwa kwa jina la kigiriki "Artemi". Diana alikuwa miungu ya uongo ya kurutubisha uzazi.

kuliinuka mvurugano mkubwa

"Watu walikuwa wamechanganyikiwa kabisa"

njia

Hili lilikuwa ni neno lililotumika kutaja Ukristo.

Sonara fulani aliyekuwa akiitwa Demetrio

Matumizi ya neno "fulani" linamwelezea mtu mpya katika habari.

Mfua fedha

Mtu mjuzi anayefanya kazi ya kufua fedha kufanya visanamu na vito vya thamani.

aitwaye Demetrio

Hili ni jina la mtu mwanaume. Demetrio alikuwa mfua dhahabu katika Efeso aliyekuwa kinyume na Paulo na kanisa la mtaa hapo Efeso.

alizalisha fedha nyingi kwa biashara hiyo

"aAlitengeneza pesa nyingi kutoka kwa watu waliotengeneza visanamu.

Acts 19:26

Sentensi unganishi

Demetrio anaendelea kuzungumza na mafundi

munaona na kusikia kwamba

"Mumekuja kwa kujua na kuelewa kwamba"

kuwageuza watu wengi

Paulo anawazuia watu kuacha kuabudu miungu. Paulo anawashawishi watu kufuata mwelekeo mwingine.

Anawaeleza kuwa hakuna miungu ambayo iliyotengenezwa kwa mikono

Neno hapa "Mikono" linaelelzea hali yote ya mtu. Anamaanisha kuwa Hakuna miungu iliyotengenezwa kwa mikono ya wanadamu iliyo ya kweli.

kwamba biashara yetu haitaweza kuhitajika tena.

"Kwamba watu hawataweza tena kuhitaji na kununua miungu kutoka kwetu."

hekalu la mungu mkuu mke diana hataonekana na thamani tena.

Hii inaweza kutafsiriwa kuwa; "watu watafikiri kuwa hakuna faida inayoendelea kuabudu katika hekalu ya mungu mke Diana."

Hata atapoteza umaarufu wake

Umarufu wa Diana utapotea kwa kufikiri habari yake.

ambao wote walio Asia na ulimwengu wa waabuduo

hili linakuzwa ili kuonyesha vile Diana alivyokuwa anapendwa na wengi.

Acts 19:28

Taarifa ya jumla

Habari hii inazungumzia mafundi waliokuwa wakifua visanamu. Kundi jingine ni la wale waliokusanyika kuwasikiliza mafunzi wafua visanamu.

Taarifa ya jumla

Gayo na Aristariko walitoka Makedonia lakini walikuwa wakitenda kazi na Paulo katika Efeso katika wakati wake.

walijawa na hasira

"wakawa na hasira sana"

na wakapiga kelele, wakisema

kelele kwa sauti kubwa, akizungumza

Mji wote ulijawa na taharuki

Watu waliokuwemo katika mji wote wakaingiwa na taharuki na kuanza kupiga kelele.

watu wakakimbia kwa pamoja

Kulikuwa na hamasisho la ghasia kubwa

kwenye ukumbi

Ukumbi wa Efeso ilitumika kwa ajili ya mikutano ya hadhara na kwa ajili ya burudani kama vile michezo na muziki

Washirika walioambatana na Paulo

watu waliokuwa wakisafiri pamoja na Paulo

Gayo na Aristarko

Haya ndiyo majina ya watu wanaume

Acts 19:30

Taarifa ya jumla

Efeso ilikuwa sehemu ya utawala wa Rumi katika jimbo la Asia.

kuingia kwenye ukumbi

Ukumbi wa Efeso ulitumika katika mikutano ya wazi na kwa matamasha ya michezo na muziki. Ulikuwa ni ukimbi inje ya mji wenye nusu mduara ukiwa na viti vyenye kubeba watu maelfu.

Acts 19:33

Alexazanda

Hili ni jina la mtu mwanamme

akawapungia mkono ili kuelezea

kutigisha mkono akitoa ishara kwa watazamaji ili wanyamaze na aweze kutoa maelezo.

kufanya maelezo

Alitaka kutoa hotuba, lakini sio wazi nini alichokuwa anakwenda kusema.

bila ya sauti

Kupaza sauti ya watu wote kwa wakati mmoja ilionekana kama sauti moja ikinena.

Acts 19:35

Sentensi jumuishi

Karani wa mji anaongea ili kuunyamazisha umati wa watu

Karani wa Mji

Hii inafafanua juu ya "Karani" au "Mwandishi"

Je, kuna yeyote ambaye hajui kuwa mji wa Efeso ni hekalu mlinzi wa Diana mkuu na ya sanamu iliyoanguka kutoka mbinguni

karani aliuliza swali hili kuwahakikishia umati kuwa walikuwa sahihi na kuwatia moyo.

Nani asiyejua

Karani wa mji anatumia neno "asiye" ili kusisitiza kuwa watu wote wa mji wanajua hili.

Mlinzi wa hekalu

Watu wa Efeso wanatunza na kulinda hekalu la Atemi

sanamu iliyoanguka kutoka mbinguni

Ndani ya hekalu la Diana kulikuwa mfano wa mungu fasheni iliyoanguka kutoka angani, kulikuwa mwamba uliofikiriwa kutoka Zeus

Acts 19:38

Sentensi unganishi

karani wa mji alimaliza kizungumza na umati

Kwa sababu hiyo

Hili neno linaashiria kuwa Karani alisema kwa sababu ya kile ambacho alisema hapo awali. Karani wa mji alikuwa amesema, Gayo na Aristariko alikuwa walikuwa si wezi wala wenye kufuru.

wanamashitaka dhidi ya mtu yetote

Nono "shitaka" na "tuhumu" ni vitendo dhidi ya wengine.

Liwali

Huyu alikuwa ni gavana, mwakilishi wa mambo ya kisheria katika mahakama.

Acha washitakiane wao kwa wao

Hili halimaanishi Demetrio na wale waliokuwa naye watashitakiana wao kwa wao. Hili lilikuwa eneo ambalo kila mtu alikuwa huru kutoa shitaka kwa mtu yeyote.

Lakini kama wewe ukitafuta chochote kuhusu mambo mengine

"Lakini kama kuna matatizo vema kuongea"

yatashughurikiwa katika kikao halali.

"Vema kujadili na kutatua tatizo kwa utaratibu wa kawaida"

katika hatari ya kutuhumiwa kuhusu ghasia siku hii.

"Hii inaweza kusababisha hatari kwa mamlaka ya Rumi tukituhumiwa kuanzisha ghasia kama hii ya leo"

Acts 20

Matendo 20 Maelezo kwa jumla

Muundo na Mpangilio

Katika sura hii Luka anafafanua safari ya mwisho ya Paulo kwa waumini walioko katika mikoa ya Makedonia na Asia kabla ya Paulo kurudi Yerusalemu.

Dhana maalum katika sura hii

Kupiga mbio

Paulo alifananisha maisha ndani ya Yesu kan kwamba alikuwa kwa mashindano ya kupiga mbio. Alimaanisha kwamba alihitaji kuendelea kufanya bidii sana hata kama mambo hayakumwendea vyema mpaka akataka kuachia njiani. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#discipline)

"Kulazimishwa na Roho"

Paulo alifikiri kwamba Roho Mtakatifu alimhitaji aende Yerusalemu hata kama yeye hakutaka. Huyo Roho Mtakatifu pia aliwaambia watu wengine kwamba Paulo atakapofika Yerusalemu watu watajaribu kumdhuru.

<< | >>

Acts 20:1

Taarifa unganishi

Paulo anaondoka Efeso anaendelea safari zake

baada ya ghasia

"Baada ya ghasia" au "kufuatia ghasia"

Aliwaaga

"alisema kwaheri."

aliwatia moyo waumini sana

"Kwa hali ya dhati aliwatia moyo waumini" au "Alisema mambo mengi ya kuwatia moyo waumini"

Baada ya kuishi miezi mitatu huko

yeye alikaa miezi mitatu huko

njama iliandaliwa dhidi yake na Wayahudi

"Wayahudi waliandaa njama dhidi yake"

wakati alipokuwa karibu kusafiri kwa meli kuelekea Syria

alikua tayari kusafiri kwa meli kwenda Syria

Acts 20:4

Taarifa ya jumla

Luka mwandishi wa Matendo ya Mitume, alikuwa ameungana na timu ya Paulo. Hapa anatumia maneno ya wingi akimtaja Paulo akiwamo na yeye.

kuandamana naye

Kusafiri pamoja na Paul

Sopatro ... Trofimo

Haya ndiyo majina ya watu wanaume

Berea ... Derbe ... Troa

Haya ndiyo majina ya maeneo waliyopitia

Aristarko ... Gayo

Haya ni majina ya watu wanaume

Watu hawa walikuwa wamekwenda mbele yetu

"hawa watu walikuwa wamesafiri mbele yetu"

siku za mikate isiyotiwa chachu

Hii inaelezea juu ya wakati wa sikukuu ya Wayahudi. Kipindi cha Pasaka.

Acts 20:7

Taarifa unganishi

Luka anaelezea huduma ya Paulo ya mahubiri huko Troa na kile kilichotokea juu ya Eutiko

Taarifa ya jumla

Luka bado anaelezea kuwa walikuwa pamoja katika safari hiyo.

kumega mkate

Mkate kilikuwa ni chakula cha kawaida wakati wa saa ya chakula. Kumega mkata hapa, inaweza kuwa walishiriki chakula saa ya chakula.

aliendelea kunena

aliendelea kutoa ujumbe

Chumba cha juu

Hii inaweza kuwa chumba cha juu ghorofa ya tatu.

Acts 20:9

Taarifa ya jumla

Habari hii inazungumzia juu ya Paulo na Eutiko.

katika dirisha

Hii ilikuwa sehemu ya uwazi katika kona ya ukuta wa chumba cha juu. Upana wake ulitosha mtu kuweza kuketi pale.

Eutiko

Hili ni jina la mtu mwanaume

aliyepatwa na usingizi mzito

Hapa inasemea; "Alichoka sana na kupelekea usingizi mzito uliompata"

ghorofa ya tatu na aliokotwa akiwa amekufa

Wakati walipotelemka kwenda kuona hali yake, walimwona akiwa amekwisha kufa.

Ghorofa ya tatu

Hii inamaanisha ghorofa mbili kabla ya tatu inayofuata.

Acts 20:11

Taarifa unganishi

Huu ni mwisho wa sehemu ya hadithi kuhusu mahubiri ya Paulo kule Troa na kuhusu Eutiko

waliumega mkate

Mkate kilikuwa chakula cha kawaida kipindi cha saa ya chakula. Inamaanisha pengine walishiriki chakula kilichokuwa na aina nyingi zaidi ya mkate.

aliondoka

"aliendelea na safari"

Mvulana

Inawezekana kuwa na maana ya; 1) kijana zaidi ya 14, au 2) mtumishi au mtumwa au 3) mvulana kati ya umri wa 9 na 14 miaka.

Acts 20:13

Taarifa unganishi

Paulo na wenzake wakaendelea na safari yao

Taarifa ya jumla

Fungu hili linazungumzia juu ya Luka na wale waliokuwa wakisafiri naye bila Paulo kuwemo kwenye kundi.

Sisi wenyewe tulikwenda

Neno 'wenyewe' linaongeza mkazo na hutenganisha Luka na wasafiri wenzake Paulo, ambaye hakusafiri kwa mashua

tulisafiri kwenda Aso

Aso ni mji uliokuwa chini ya mji wa Behram ya sasa katika Uturuki pwani ya bahari ya Aegean.

yeye mwenyewe alitamani

"yeye mwenyewe" ni kiwakilishi cha jina la Paulo aliyekuwa anatamani

kwenda kwa njia ya bara

Kusafiri kwa nchi kavu

kwenda Mitylene

Mitylene ni mji katika siku ya leo Mitilini, Uturuki katika pwani ya bahari ya Aegeana.

Acts 20:15

Taarifa ya jumla

Habari hii inaelezea Paulo, Mwandishi Luka na wale waliosafiri pamoja nao.

upande wa pili wa kisiwa

"karibu na kisiwa" au " kuvuka kutoka kwenye kisiwa"

Kisiwa cha Chiosi

Chiosi ni kisiwa katika pwani ya Uturuki kwa sasa katika bahari ya Aegean

tulitia nanga kisiwani cha Samos

"Tuliwasili katika kisiwa cha Samos"

kisiwa cha Samos

Samos ni kisiwa cha kusini ya Chios katika pwani ya bahari ya Aegean kwa sasa ni Uturuki.

mji wa mileto

Mileto ulikuwa ni mji wa bandari magharibi mwa Asia Ndogo karibu ni kwenye chanzo cha mto Meander.

Paulo alikuwa ameamua kusafiri kupitia Efeso

Paulo alisafiri majini kusini zamani mji wa bandari wa Efeso, kusini zaidi ili kufika nchi kavu huko Mileto.

ili kwamba asitumie muda wowote

Hii inamaanisha "muda" kama vile ulikuwa bidhaa ambao mtu angeweza kuutumia.

Acts 20:17

Taarifa unganishi

Paulo anawaita wazee wa kanisa la Efeso na kuanza kuzungumza nao.

kutoka Mileto

Mileto ilikuwa ni mji wenye bandari Magharibi ya Asia ndogo karibu na chanzo cha mto Meander.

Ninyi wenyewe

Paulo hapa anatumia msisitizo kwa kile anachowaambia.

kuweka mguu katika Asia

aliingia mkoa huu wa Asia

jinsi nilivyokuwa kwenu muda wote

Anazungumzia muda alioutumia akiwa kwao.

kwa unyenyekevu wote

'Unyenyekevu' au 'kujishusha hadi chini'

kwa machozi

"machozi" wakati mwingine alijisikia hali ya huzuni na kulia machozi.

kwa Wayahudi

Hii haimaanishi kwa kila Myahudi. Anaelezea juu ya baadhi ya wale waliomtendea mabaya.

Mwajua jinsi ambavyo sikujizuia kutangaza kwenu

" Mnajua jinsi ambavyo sikunyamaza, lakini kila mara niliwahutubia."

kwenda nyumba kwa nyumba

Paulo alifundisha watu kwenye makazi yao binafsi yaani nyumba kwa nyumba.

juu ya toba kwa Mungu na imani katika Bwana wetu Yesu

"toba" na "imani" ni maneno yanayoweza kutafsiriwa kwa vitenzi. Kwamba walipaswa kutubu mbele za Mungu na kuamini katika Bwana Yesu Kristo.

Acts 20:22

nikiwa ninamtii Roho Mtakatifu kuelekea Yerusalemu, nisiyajue mambo ambayo yatanitokea mimi huko,

Hapa anaongelea juu ya Roho Mtakatifu akimshawishi Paulo kwenda Yerusalemu kama vile Roho Mtakatifu alikuwa amemfunga mfano wa mtumwa.

Roho Mtakatifu hunishuhudia mimi

Roho Mtakatifu amewasilisha maonyo haya kwangu

minyororo na mateso ndivyo vinavyoningojea

Mimi nahusika kufungwa jela kwa minyororo na kuteswa katika kifungo.

ili niweze kumaliza mwendo wangu na huduma niliyopokea kutoka kwa Bwana Yesu

Paulo anatumia mfano waq mashindano. Ili kukamilisha kazi ambayo Mungu aliiweka kwa ajili ya yake kuifanya

kuishuhudia injili ya neema ya Mungu

"kuwaambia watu habari njema kuhusu neema ya Mungu. Hii ndiyo huduma ambayo Paulo alikuwa ameipokea kutoka kwa Yesu.

Acts 20:25

Taarifa unganishi

Paulo anazidi kuongea na wazee wa Efeso

Na sasa, tazama, najua

"Na sasa, nisikilizeni kwa makini, kwasababu ninajua"

Mimi najua kuwa ninyi nyote

Mimi najua kuwa ninyi kwa ujumla wenu wote.

miongoni mwao nilikwenda kuwahubiri kuhusu Ufalme

kwenu ambao mimi niliwahubiria ujumbe kuhusu ufalme wa Mungu

hamtaniona uso wangu tena

Neno 'uso' hapa inawakilisha mwili wa Paulo.

Mimi sina hatia katika damu ya mtu yoyote

Siwezi kulaumiwa na mtu yeyote kuwa na hatia mbele za Mungu

mtu yeyote

Hapa inamaanisha nafsi ya kila mmoja wao awe mwanaume au mwanamke.

Kwa maana sikujizuia kuwatangazia

"kwamba sikukaa kimya bila kuwatangazia ujumbe wa kweli.

Acts 20:28

Kwa sababu hiyo

Neno hili ni alama ya kauli inayosema kwa sababu ya kile ambacho nilisema hapo awali. Katika kesi hiyo, inaturudisha nyuma kwa yale yote ambayo Paulo amesema hadi sasa katika hotuba yake kuhusu yeye kuondoka kwao.

juu ya kundi lolote ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi. Iweni waangalifu kulichunga kusanyiko la Bwana

Waumini wanafananishwa na kundi la kondoo. Viongozi wamepewa wajibu na Mungu kulilinda kundi la waumini kwa uangalifu mkuu dhidi ya mbwa mwitu.

kusanyiko la Bwana, ambalo alilinunua kwa damu yake mwenyewe

kumwaga "damu" ya Kristo hapa inafananishwa na malipo kwa Mungu kwa ajili ya dhambi zetu.

mbwa mwitu wakali wataingia kwenu, na wasilihurumie kundi.

Ni picha ya waumini ambao ni kondoo kuanza kufundishwa mafundisho ya uongo yatakayoanza kuwavutana kuwatoa katika kweli ya Mungu

ili kuwavuta wanafunzi wawafuate wao

Mwalimu wa uongo anayeweza kuwavuta waumini kwa mafundisho ya uongo, kwa lengo la kuwaondoa waumini kuwa wanafunzi wa Yesu na kuwafanya kuwa wanafunzi wake.

Acts 20:31

kuwa macho. kumbuka

'kuwa macho na kukumbuka' au 'kuwa macho kama unakumbuka' au 'kuwa macho kwa kukumbuka.'

Kuwa macho

kuwa macho na tahadhari 'au' kuangalia nje" au "kukaa macho"

Kumbuka

"Endelea kukumbuka" au "Tahadhari"

kwa miaka mitatu sikuweza kuacha kuwafundisha... usiku na mchana

Paulo hakufuruliza kuwafundisha kwa miaka mitatu, lakini mara kwa mara katika muda wa miaka mitatu.

Sikuweza kuacha kuwafundisha

Maana inawezekana ni 1) 'sikuweza kuacha kuwaonya au 2) "sikuweza kuacha kuhamasisha kwa marekebisho."

kwa machozi

Hapa "machozi" inaelezea kilio cha Paulo kwasababu ya hisia zake kali juu ya vile alivyojihisi wakati akiwaonya hao watu.

Na sasa mimi nawakabidhi kwa Mungu, na kwa neno la neema yake

Hapa "neno" linasimama juu ya ujumbe. Kwamba namwomba Mungu awalinde na kuwasaidia kuendelea kuuamini ujumbe niliosema nanyi juu ya neema yake.

ambalo laweza kuwajenga

Imani ya mtu kuwa imara ni mfano wa ukuta uliojengwa na kuzidi kuimarishwa zaidi na zaidi.

na kuwapa urithi

Hapa pia anazungumzia neno la neema yake Mungu kana kwamba Mungu mwenyewe alikuwa akiwapa urithi watu wake.

Acts 20:33

Taarifa unganishi

Paulo alimaliza hotuba yake kwa wazee wa Kanisa la Efeso, Ambayo alikuwa akiihutubia

Sikutamani fedha ya mtu.

"Sikuwa na tamaa ya fedha za mtu yeyote" au "Mimi mwenyewe sikuhitaji fedha ya mtu yeyote"

fedha ya mtu, dhahabu, au nguo

Mavazi yalidhaniwa kuwa kama hazina; kwa kadri mtu alivyozidi kuwa navyo, ndivyo alivyodhaniwa kuwa na utajiri.

Ninyi wenyewe

Neno "wenyewe" inatumika hapa kwa kuongeza msisitizo.

nimefanya kazi kwa mikono yangu mwenyewe kutimiza mahitaji yangu.

Neno "mikono" hapa inawakilisha roho yote ya Paulo. 'Mimi nilifanya kazi kwa mikono yangu mwenyewe ya kupata fedha na kulipa kwa ajili ya gharama zangu."

Kufanya kazi kuwasaidia wanyonge

"Fanyeni kazi ilikupata fedha kusaidia watu ambao hawawezi kuzipata kwaajili yao wenyewe"

maneno ya Bwana Yesu,

Hapa "maneno" yanafafanua juu ya Yesu alivyosema.

Ni heri kutoa kuliko kupokea

Mtu hupokea neema ya Mungu na uzoefu wa furaha yake zaidi anapotoa

Acts 20:36

Taarifa unganishi

Paul anamalizia muda na hotuba yake kwa wazee wa kanisa la Efeso na kisha kuomba pamoja nao.

alipiga magoti akaomba pamoja nao

Ilikuwa desturi ya kawaida kupiga magoti wakati wa kuomba. Ilikuwa alama ya unyenyekevu mbele za Mungu.

kumwangukia Paulo shingoni

"Aliwakumbatia kwa karibu" au "kuweka mikono yao karibu naye"

walimbusu

Kumbusu mtu kwenye shavu ni usemi wa kindugu au upendo wa kirafiki katika Mashariki ya Kati.

Kamwe hawatauona uso wake tena

Neno "uso" hapa inawakilisha mwili wa Paulo kimwili. 'hamtaniona katika mwili katika dunia hii.'

Acts 21

Matendo 21 Maelezo kwa Jumla

Muundo na Mpangilio

Matendo 21:1-19 Inaelezea safari ya Paulo kwenda Yerusalemu. Baada ya kuasili Yerusalemu,Waumini walimuambia kwamba Wayahudi walitaka kumdhuru .Walimwelezea pia alichopaswa kufanya ili wasimdhuru (Mistari 20-26). Ingawa Paulo alikifanya alichoambiwa na waumini,Wayahudi walijaribu kumuua. Warumi walimuokoa na wakampa nafasi ya kuwaongelesha Wayahudi.

stari wa Mwisho wa sura hii unaishia na sentensi isiyokamilifu kimaana. Tafsiri nyingi huwacha hiyo sentensi kama haijakamilika kama vile ULB hufanya.

Dhana maalum katika sura hii

"Wote wamejitahidi kuilinda sheria"

Wayahudi wa Yerusalemu walifuata sheria za Musa. Hata wale waliomfuata Yesu bado walizizingatia. Makundi yote yalifikiri kwamba Paulo alikuwa akiwaambia Wayahudi walio Uyunani wasifuate hizo sheria. Lakini watu wa Mataifa ndio Paulo alikuwa akiwahutubia.

Nadhiri za kuwafunga wanaume

Nadhiri ambazo Paulo na marafiki wake watatu walichukua ilikuwa ni kama ya Wanaume wa kujifunga kwa Nadhiri kwa vile walinyoa nywele zao (Matendo 21:32)

Watu wa Mataifa kwa hekalu

Wayahudi walimlaumu Paulo kwa kumleta mtu wa Mataifa katika sehemu maalum ya hekalu ambamo Mungu aliwaruhusu Wayahudi pekee kuingia. Wakafikiri kwamba Mungu alitaka wamuadhibu Paulo kwa kumuua. (Tazama: //en/tw/dict/bible/kt/holy)

Uraia wa Urumi

Warumi walidhani kwamba ni Warumi pekee yao waliostahili kuhudumiwa kwa haki. Wangewatenda watakavyo wale ambao hawakuwa raia wa Urumi lakini kwa Warumi waliwatendea kufuata sheria. Watu wamoja walizaliwa raia wa Roma na wengine wakaipa pesa serikali ya Warumi ili wawe raia.

<< | >>

Acts 21:1

Sentensi unganishi

Mwandishi Luka, Paulo na washirika wake wanaendelea na safari yao.

Taarifa ya jumla

Paulo anatumia kiwakilishi cha jina kwa wingi akijitambulisha yeye, Paulo na wenzao wanaosafiri kwa pamoja.

tukafika moja kwa moja kwenye mji wa Kosi,

"tulikwenda moja kwa moja kwenye mji wa kosi" au "tulikwenda moja kwa moja kwenye mji wa kosi bila kupitia sehemu nyingine"

Mji wa Kosi

Kosi ni kisiwa cha pwani ya Ugiriki pwani kwa sasa ni Uturuki mkoa wa kusini mwa Aegean ya bahari.

Mji wa Rhodes

Rhodes ni kisiwa cha pwani ya Ugiriki kwa sasa ni Uturuki kusini mwa bahari ya Aegeani na kosi pia kaskazini ya Krete

Mji wa Patara

Patara ni mji upande wa kusini magharibi mwa pwani ya Bahari ya Aegean kwa sasa ni Uturuki kuelekea bahari ya Mediterraneani.

Tulipopata meli inayovuka kwenda Foinike

Hapa "Meri kuvuka kupitia" linamaanisha kuwa ni wale watumishi wa meri ambao wangesafiri pamoja na meri.

Meri kuvuka kupitia

Hapa hakumaanishi meri ilikuwa inavuka wakati huo, bali ingevuka baadaye.

Acts 21:3

Taarifa ya jumla

Neno 'sisi' linamhusu Luka, Paulo na wale waliokuwa wakisafiri pamoja nao.

tukaiacha upande wa kushoto

"Tulikipita kisiwa upande wa kushoto"

huko ndiko meli ilikuwa ipakuliwe shehena yake

Hapa "Meri" inasimama kwa nafasi ya watumishi waliokuwa wakisafiri na meri. Wafanyakazi hao wangeshusha mizigo kutoka merini.

Wanafunzi hawa walimwambia Paulo kupitia Roho

"Waumini hawa walimwambia Paulo kile Roho Mtakatifu alikuwa amekidhihirisha kwao"

kwamba yeye asikanyage Yerusalemu

Hapa "Miguu" linamaanisha Paulo mwenyewe asikanyage huko Yerusalemu.

Acts 21:5

Taarifa ya jumla

Fungu hili linazungumzia waumini huko Tiro

Wakati tulipokuwa tumekaa siku kadhaa

Inaonyesha kuwa kuna muda waliokaa katika mji huo.

tukapiga magoti pwani, tukaomba

likuwa desturi ya kawaida kupiga magoti wakati wa kuomba. Hii ilikuwa ni alama ya kuonyesha unyenyekevu mbele za Mungu.

tukaagana kila mmoja

"Alisema 'kwaheri' kwa kila mmoja

Acts 21:7

Sentensi unganishi

Paulo anaanza rariba yake akiwa Kaisaria

tuliwasili Tolemai

Tolemai ulikuwa ni mji wa kusini mwa Tiro, Lebanoni. Tolemai ya sasa ni Acre, Israeli.

ndugu hawa

"waumini wenzake"

mmoja kati ya saba

"Saba" inahusu wanaume waliochaguliwa kusambaza chakula na misaada kwa wajane.

mtu huyu

"Philipo"

Sasa

Neno hili limetumika kama alama ya kumalizika kwa tukio moja na kuanza kwa tukio jingine. Luka anasimulia habari za Philipo na binti zake.

mabinti wanne mabikira ambao walitabiri

"Mabinti bikra wanne ambao kwa kawaida walikuwa wakipokea na kupeleka ujumbe kwa watu kutoka kwa Mungu.

Acts 21:10

Sentensi unganishi

Fungu hili linazungumzia habari ya unabii ulionenwa kumhusu Paulo katika Kaisaria kutoka kwa nabii Agabo.

nabii mmoja aitwaye Agabo

Hii inamtambulisha mtu mpya katika habari hii.

Agabo

Agabo alikua mtu kutoka Yudea

Kuchukua mkanda wa Paulo

"Aliutwaa mkanda wa Paulo kutoka kiunoni mwake"

na kusema, "Roho Mtakatifu asema hivi," "Wayahudi wa Yerusalemu watamfunga mtu anayemiliki mkanda huu

Alimaanisha kuwa Roho Mtakatifu alimjulisha Nabii Agabo kuwa Wayahudi huko Yerusalemu watamfunga Paulo kama alivyojifunga mkanda wa Paulo na kumkabidhi kwa watu wa mataifa.

Wayahudi

Hii haimanishi Wayahudi wote, lakini baadhi ya watu walifanya hivyo.

kumkabidhi mikononi mwa

"Kumkabidhi kwa"

katika mikono ya wamataifa

Neno "Mikono" Linawakirisha udhibiti.

Wamataifa

Neno hili linasimamia mamlaka miongoni mwa wamataifa.

Acts 21:12

Taarifa ya jumla

Fungu hili linaelezea kumhusu Mwandishi Luka na baadhi ya waumini isipokuwa Paulo.

Mnafanya nini, mnataka kuvunja moyo wangu?

Paulo anauliza swali hili kuonyesha waumini wanapaswa kuacha kujaribu kumshawishi. 'Acheni, mnachofanya mnataka kunivunja moyo wangu.'

Kwa jina la Bwana Yesu

Hapa "jina" linamaanisha utu wa Yesu Kristo.

hakutaka kushawishiwa

Hakuweza kujaribu kumshawishi ili asiende Yerusalemu.

mapenzi ya Bwana yafanyike

Inamaanisha kuwa; lolote lile likitokea litakuwa kwa mpango wa Bwana.

Acts 21:15

Sentensi unganishi

Huu ni mwisho wa kipindi cha Paulo kuwa huko Kaisaria.

Taarifa ya jumla

Neno 'sisi' linamhusu Luka, Paulo na wale waliosafiri pamoja nao.

Pamoja walimleta mtu

"Miongoni mwao alikuwemo mtu mwingine"

Mnasoni, mtu kutoka Kupro

Mnasoni alikuwa mtu kutoka kisiwa cha Kupro.

mwanafunzi wa kwanza

Hii inamaanisha Mnason alikuwa muumini wa Yesu aliyeamini mwanzoni mwa huduma.

Acts 21:17

Sentensi unganishi

Paulo na wenzake sasa wanafika Yerusalemu.

ndugu walitukaribisha

Hawa walikuwa waumini wanaume na wanawake, waliowakaribisha.

alitoa taarifa hatua kwa hatua

"Paulo alitoa maelezo ya kina ya mambo yote ambayo Mungu aliyatenda"

Acts 21:20

Sentensi unganishi

wazee katika Yerusalemu wakaanza kumjibu Paulo.

ndugu

Neno "ndugu" linamaanisha waumini wenzao.

Wameambiwa kuhusu wewe... wasifuate desturi za zamani.

Hapa baadhi ya Wayahudi walikuwa wakifuatilia kuharibu mafundisho ya Paulo aliyokuwa amawafundisha waumini wapya, ili wafuate desturi za Musa badala ya kumfuata Yesu.

Wameambiwa

"Watu waliwaambia waumini wa Kiyahudi"

Acts 21:22

Taarifa ya jumla

Fungu hili limawahusu Yakobo na wazee wengine.

watu wanne ambao waliweka kiapo

Hii ilikuwa ni aina ya kiapo ambapo mtu hakutaka kunywa kileo au kukata nywele zao mpaka mwisho wa kipindi cha kuweka muda. "watu wanne ambao walitoa ahadi kwa Mungu."

Wachukue watu hawa na ujitakase mwenyewe pamoja nao

Walikuwa wanapaswa wao wenyewe kujitakasa ili waweze kuabudu ndani ya hekalu.

na uwalipie gharama zao

Lipa kile ambacho watahitaji kulipiwa.

ili waweze kunyoa vichwa vyao

Hii ni ishara ya mtu anayetimiza nadhili yake kwa Mungu.

mambo waliyoambiwa kuhusu wewe

Mambo ambayo yanasemwa na watu kukuhusu wewe.

Kufuata sheria

Inamaanisha utii wa kuzishika sheria za Mungu.

Acts 21:25

Sentensi unganishi

Yakobo na Wazee katika Yerusalemu wanamaliza maswali yao kwa Paulo.

wanapaswa kujiepusha na vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu, na damu, kutokana na kile kilichonyongwa

ote hayo yalikuwa sheria za kile wanachotakiwa kula.

kujiepusha na vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu

Wajiepushe kula nyama iliyotolewa kwa ibada za sanamu.

kutokana na kile kilichonyongwa

Mnyama ambaye ameuawa bila damu kutoka.

ibada ya kujitakasa pamoja nao

Kabla ya kuingia Hekaluni Wayahudi walitakiwa kuwa sherehe au tohara. Kusafishwa alikuwa na kufanya na Wayahudi kuwa na mawasiliano na watu wa mataifa mengine.

siku ya kujitakasa

Hii ni hatua tofauti ya kujitakasa ambayo ilitakiwa kuitimiza ili waweze kuingia hekaluni.

mpaka sadaka ilipotolewa

"Mpaka walipowasilisha wanyama kwa sadaka"

Acts 21:27

Sentensi unganishi

Huu ni mwanzo wa sehemu ya hadithi kuhusu kukamatwa kwa Paulo.

Taarifa ya jumla

Mstari wa 29 unaelezea habari kuhusu Wayahudi kutoka Asia.

Siku saba

Hizi zilikuwa siku saba kwa ajili ya kujitakasa.

katika Hekalu

Paulo hakuwa ndani ya hekalu lenyewe. Alikuwa kwenye uwa wa nje wa hekalu.

Makutano wote wakashawishika

"Ilisababisha kundi kubwa la watu kuanzisha upinzani.

na wakamnyoshea mikono

Neno Kumnyoshea mikono" lina maana ya watu kuanza kumvamia.

watu, sheria na mahali

"Watu wa Israel, sheria ya Musa, na hekalu

mwanzoni walikuwa wamemwona...walidhani kwamba Paulo alikuwa ameingia na Myunani hekaluni

Mwandishi Luka anaelezea kwanini wayahudi kutoka Asia walimshitaki Paulo kuwa alimleta Myunani

Trofimu

Huyu alikuwa mwanaume Myunani ambaye Paulo alishitakiwa kuwa aliingia naye hekalu

Acts 21:30

Mji wote ulikuwa na taharuki

Neno "wote" hapa ni lugha ya kuumba picha kubwa kwa msisitizo. neno "mji" inawakilisha watu katika mji huo. "Watu wengi katika mji wakawa na hasira juu ya Paulo."

"Walimvamia Paulo"

Paulo alivamiwa

milango mara ikafungwa

Walifunga milango ili kwamba kusije kufanyika maandamano ndani ya hekalu.

habari zilimfikia mkuu wa kikosi cha ulinzi

afisa wa kikosi cha ulinzi au kiongozi wa askari wapatao 600

Yerusalemu yote ilikuwa katika ghasia

Neno "Yerusalemu" hapa inawakilisha watu wa Yerusalemu. neno "wote" ni msisitizo kuonyesha umati mkubwa waliokuwa wamekasirika. "wengi wa watu huko Yerusalemu walikuwa katika ghasia."

Acts 21:32

aliukimbilia umati chini

Kutoka ngome, kuna ngazi kwenda chini katika mahakama.

mkuu wa kikosi

afisa wa kikosi cha kijeshi cha Rumi au kiongozi wa askari wapatao 600

alimkamata Paulo

"Akamshika Paulo" au "Paulo alishikiriwa"

akaamuru afungwe minyororo

Aliwaagiza askari wake kumkamata na kumfunga.

kwa minyororo miwili

Hii inamaanisha kuwa Paulo alifungwa na maaskari wawili kila mmoja upande wake mmoja.

Akamuuliza yeye ni nani na amefanya nini.

Alimwuliza kuwa yeye ni nani?, Amefanya nini?

Akamuuliza yeye ni nani

Mkuu wa ulinzi anazungumza na umati, hazungumzi na Paulo.

Acts 21:34

Jemadari

Huyu alikuwa ni afisa wa kijeshi au kiongozi wa askari wapatao 600.

aliagiza Paulo aletwe ndani

Aliagiza askari wake wamlete Paulo.

ndani ya ngome

Ngome hii ilikuwa imeunganishwa kwenye uwanda wa nje wa hekalu.

Wakati alipofika kwenye ngazi, walimchukua

'Wakati Paulo alipofika kwenye ngazi za ngome, askari wakamchukua'

Muondoeni huyu

Umati wa watu kwa kutumia lugha kiasi fulani kali na lugha halisi ya kuomba Paulo auwawe.

Acts 21:37

Paulo alipokuwa analetwa

"askari walipokuwa tayari kuleta Paulo"

Ngome

ngome ilikuwa imeunganishwa na uwanda wa nje wa hekalu

mkuu wa kikosi cha ulinzi

afisa wa jeshi la Kirumi wa askari wapatao 600.

Je, unajua Kiyunani? Wewe si yule Mmisri ambaye awali aliongoza uasi na alichukua magaidi elfu nne nyikani?

Mkuu wa jeshi anatumia maswali haya kueleza mshangao kwamba Paulo si yule aliyemdhani kuwa. Nilifikiri kuwa ni yule Mmisri ambaye aliongoza uasi katika jangwa na magaidi elfu nne."

wewe si yule Mmisri

Muda mfupi kabla ya ziara ya Paulo, mtu asiyejulikana jina kutoka Misri, alikuwa akizindua uasi dhidi ya Rumi katika Yerusalemu. Baadaye alitorokea "jangwani," 'na kamanda anashangaa kama Paulo atakuwa ndiye na mtu huyo.

aliongoza uasi

Neno "uasi" linamaanisha watu waliasi na kwenda kinyume na serikali ya Rumi"

magaidi elfu nne

"4000 watu wanaoua na kuwadhuru wengine wale wasiokubaliana nao"

magaidi

Ni wale Wayahudi walioiasi serikali ya Rumi na kuanza kuwauaWarumi na kila mmoja ambaye aliyeunga mkono serikali ya Kirumi.

Acts 21:39

Sentensi unganishi

Paulo anaanza kujitetea kwa kile alichukuwa amefanya

Nakuuliza

"nakuomba" au "nakusihi"

nikubalie

"Tafadhali nikubalie" au tafadhali niruhusu"

Jemadari alikuwa amempa kibali

Neno "kibali" linamaanisha kuwa mkuu wa kikosi alikmpa Paulo kibali cha kuzungumza.

Paulo akasimama penye ngazi

Neno "ngazi" linamaanisha hatua ya juu ya kupanda kuelekea kwenye ngome.

akatoa ishara ya mkono kwa watu

Paulo alitoa ishara ya mkono kwa watu kuashiria wanyamaze

kulipokuwa na ukimywa sana

wakati watu waliponyamaza kabisa

Acts 22

Matendo 22 Maelezo kwa Jumla

Muundo na Mpangilio

Hii ndio mara ya pili kusema habari ya Kubadilishwa kwa Paulo kuwa Mkristo katika kitabu cha Matendo.Kwa sababu hili ni tukio muhimu katika kanisa la awali, "kuna mara tatu ya kusema habari ya kubadilishwa kwa Paulo kuwa Mkristo. (Tazama: Matendo 9 na Matendo 26).

Dhana maalum katika sura hii

Katika lugha ya Kihebrania

Wakati huu Wayahudi wengi walizungumza Kiaramea na Kiyunani. Wengi wa waliozungumza Kihebrania walikuwa Wayahudi watu wa elimu. Hii ndio maana watu walimsikiliza Paulo kwa makini alipoanza kuzungumza kwa Kihebrania.

"The Way"

Hakuna anayefahamu aliyeanza kuwaita Waumini wafuasi wa Njia. Labda Waumini walijiita hivyo kwa vile Bibilia kwa mara nyingi humzungumzia mtu anayeishi maishi yake kama mtu atembeaye njiani. Kama huu ni ukweli, Waumini walikuwa "Wakifuata njia ya Bwana" kwa kuishi kwa njia inayompendeza Mungu.

Uraia wa Urumi

Warumi walidhani Kwmaba ni Warumi pekee yao waliostahili kuhudumiwa kwa haki. Wangewatenda watakavyo wale ambao hawakuwa raia wa Urumi lakini kwa Warumi waliwatendea kufuata sheria. Watu wamoja walizaliwa raia wa Roma na wengine wakalipa pesa serikali ya Warumi ili wawe raia. "Kiranja Mkuu" angeadhibiwa kwa kuwatendea raia wa Urumi sawa wale wasiokuwa raia.

<< | >>

Acts 22:1

Sentensi unganishi

Paulo anazungumza na Wayahudi huko Yerusalemu.

Ndugu na baba zangu

Hii ilikuwa ni njia ya kistaarabu ya kuzungumza na watu ambao walikuwa na umri sawa na wa Paulo, na wanaume wazee waliokuwa katika kusanyiko hilo.

Nitakao ufanya kwenu sasa

"Nitakaoueleza kwenu" au "nitakao uwakilisha kwenu"

Lugha ya kihebrania

"lugha ya Kihebrania ilikuwa lugha ya Wayahudi"

Acts 22:3

nilipata elimu katika mji huu, miguuni pa Gamalieli

alikuwa mwanafunzi wa rabi Gamalieli hapa Yerusalemu "

Gamarieli

Gamarieli alikuwa mwalimu mashuhuri wa sheria ya Kiyahudi.

Nilifundishwa kulingana na njia sahihi ya sheria za baba zetu.

"Aliniagiza jinsi ya kutii kwa makini kila sheria ya baba zetu" au "mafundisho niliyopata yalifuatiwa na maelezo halisi ya sheria ya baba zetu"

Nina bidii kwa Mungu

"Nimejitoa kikamilifu kumtii Mungu" au "Mimi nina hamu kuhusu huduma yangu kwa Mungu"

kama ninyi nyote mlivyo leo

"Kama ilivyo kwenu nyote hivi leo". Paulo anajilinganisha na umati wa watu.

njia hii

Hii ilikuwa ni neno lililotumika kutaja Ukristo

hadi mauti

"mauti" inaweza kutafsiriwa na kitenzi "kuua" au "kufa

na kuwatupa gerezani

"Walitupwa gerezani" au "Kuwaweka gerezani"

kutoa ushahidi

"Kushuhudia" au "kutoa ushahidi"

nilipokea barua kutoka kwao

"Makuhani wakuu na wazee nilipokea barua kutoka kwao"

kwa ajili ya ndugu zetu walioko Dameski

Hapa "ndugu" inahusu "Wayahudi wenzake

Ilikuwa niwalete Yerusalemu watu wa njia ile

"Waliniagiza kuwafunga minyororo wale wote wa njia ile na kuwaleta Yerusalemu

ili waadhibiwe

"ili wapate adhabu" au "ili viongozi wa Wayahudi wangeweza kuwaadhibu"

Acts 22:6

Sentensi unganishi

Paulo anazungumzia namna alivyoweza kukutana na Yesu.

Ikatokea ya kwamba

Msemo huu umetumika hapa kama tukio la kwanza. Hapa Paulo anaelezea jinsi alivyokutana na Yesu.

nikasikia sauti ikiniambia

Hapa "sauti" inasimama kwa mtu akizungumza. "Mimi nilisikia mtu akiniambia"

Acts 22:9

ila hawakuielewa sauti ya yule aliye ongea na mimi

Neno "sauti" linasimama badala ya mtu anayeongea. Hawakuelewa kile yule mtu alichokuwa akiongea nami.

huko utaambiwa

"kuna mtu atakuambia" au "huko utafahamu"

Sikuweza kuona kwa sababu ya mwangaza wa ile nuru

"Niliachwa nikiwa sioni kwasababu ya uli mwanga angavu.

nikaenda Dameski kwa kuongozwa kwa mikono ya wale waliokuwa na mimi

Hapa "mikono" anasimama kwa wale waliomuongoza Paul. Hii inaweza ikaanza: "Watu waliokuwa na mimi waliniongoza kwenda Dameski"

Acts 22:12

Taarifa ya jumla

Fungu hili linazungumzia habari za Anania

Anania

Huyu si Anania aliyekufa mapema mwanzoni mwa sura ya 5:3

mtu mwema kwa mujibu wa sheria

Anania ilikuwa makini sana kuhusu kufuata sheria za Mungu.

aliyenenwa vyema na Wayahudi walioishi kule

"Wayahudi walioishi kule walinema mema juu yake"

ndugu Sauli

Hapa "Ndugu" ni njia ya kistaarabu kumuelezea mtu. "Rafiki yangu Sauli"

pokea kuona

neno "kuona" inaweza kutafsiriwa na kitenzi "kuona." "kuona tena"

muda uleule

Hii ni kawaida kama tukio lilitendeka muda mfupi baada ya kuanza kwa tukio.

Acts 22:14

Sentensi unganishi

Paulo anamalizia kuwaambia kile kilichotokea kwake huko Dameski. Ananukuu kile Anania alisema kwake. Hii ni sehemu ya hotuba ya Paulo aliyoitoa huko Yerusalemu.

mapenzi yake

"kile Mungu anapanga na kinaweza kutokea"

kusikia sauti kutoka mdomoni kwake mwenyewe

Vyote "sauti" na "kinywa" rejea kwa nayezungumza. "kumsikiliza akiongea moja kwa moja kwako"

kwa watu wote

Hapa "watu" maana yake watu wote akiwa mwanamume au mwanamke. "kwa watu wote"

Na sasa

Hapa "sasa" haina maana "wakati huu," lakini linatumika kuleta umakini na hatua muhimu ifuatayo.

ubatizwe

Hii inaweza kuanza: "naomba nikupatize" au "kupokea ubatizo"

Kuoshwa na kuondolewa dhambi zako

kama kuoshwa kwa mwili wa mtu ili kuondoa uchafu, akiliitia jina la Yesu kwa msamaha wa dhambi. Omba msamaha wa dhambi zako.

ukiliitia jina lake

Hapa "jina" ni Bwana Yesu. "wito kwa Bwana" au "kuamini katika Bwana"

Acts 22:17

Sentensi unganishi

Paulo anaanza kwa kuwaambia umati wa watu kuhusu maono yake kwa Yesu.

ikatokea kwamba

Kipengere hiki kinaweka alama ya kuonyesha kuanza kwa tukio.

Nilipewa maono

Hii inaweza ikaanza: "nilikuwa na maono" au "Mungu alinipa maono"

Nilimwona akiniambia

"Nilimwona Yesu akiniambia"

hawataukubali ushuhuda wako kunihusu mimi

"Wale ambao wanaishi Yerusalemu hawataamini kile unachowaambia kunihusu mimi"

Acts 22:19

Sentensi unganishi

Huu ni mwisho wa hotuba ya Paulo kwa umati wa Wayahudi waliokuwa kwenye ngome.

Taarifa ya jumla

Fungu hili linazungumzia Wayahudi wasioamini waliokuwa Yerusalemu

wao wenyewe wanajua

"wao wenyewe" ni msisitizo wa neno katika kiwakilishi cha jina

katika kila sinagogi

Paulo alikwenda kwenye masinagogi akiwatafuta Wayahudi waliokuwa wamemwamini Yesu.

damu ya Stefano ... ilikuwa imemwagika

Msemo huu ulikuwa ni desturi ya kusema mtu aliyeuawa. "walimwua Stephen."

Acts 22:22

Mwondoeni mtu huyu katika nchi

Neno "nchi" yanaongeza mkazo "Mwondoeni." : "Mwueni"

Na walivyokuwa

Neno "Walipokuwa" limetimika kwa alama matukio mawili ambayo yanatokea wakati huo huo.

na kutupa mavazi yao na kutupa mavumbi juu

Tukio hili linaonyesha Wayahudi walikuwa wamekasirika kwasababu walijisikia kuwa Paulo alikuwa amenena kinyume cha Mungu.

akaamuru Paulo aletwe

Hii inamaanisha "aliwaamuru askari wake ili kumleta Paulo"

ngome

ilikuwa imeungana na uwanda wa nje wa hekalu

Akaamuru aulizwe huku anapigwa mijeledi

Kamanda alitaka Paul kuteswa kwa kuchapwa viboko ili kuhakikisha anasema ukweli.

Acts 22:25

Taarifa ya jumla

Fungu hili linazungumzia juu ya askari.

Kamba

Hizi zilikuwa na nyuzi nyuzi za ngozi au mnyama.

Je, ni halali kwenu kumpiga viboko mtu ambaye ni raia wa Rumi na hajakuhumiwa bado?

Paulo alitumia swali hili kuuliza juu ya uhalali wa kuchapwa kwake viboko. "Si halali kwenu kumpiga mijeledi mtu ambaye ni raia wa Rumi na hajakuhumiwa!"

Je, unataka kufanya nini?

Swali hili limetumika kuwaomba kamanda kufikiria upya mpango wake wa kumjeledi Paulo. "Hupaswi kufanya hivi!"

Acts 22:27

Taarifa ya jumla

Fungu hili linazungumzia habari za Paulo

Jemedari mkuu akaja

Neno "kuja" linaweza kuwa na maana ya "kwenda"

ilikuwa kiasi kikubwa cha pesa

"Ilikuwa baada ya kulipa kiasi kikubwa cha pesa katika mamlaka ya Kirumi"

ndipo nilipata uraia.

"Nilijipatia uraia" au " Nilipewa uraia"

Mimi ni Mrumi wa kuzaliwa

Baba akiwa raia wa Kirumi, hivyo watoto wake wanakuwa raia wa Kirumi mara wanapozaliwa

wale waliokuwa tayari kwenda kumuuliza

Wanaume waliokuwa wamepanga kumwuliza maswali.

Acts 22:30

Taarifa ya jumla

Mstari huu unazungumzia jemedari mkuu

Jemedari mkuu

afisa wa jeshi mwenye kikosi cha askari wapatao 600

Hivyo akamfungua vifungo vyake

"yawezekana jemedaari mkuu alimfungua Paulo minyororo." au Mkuu wa jeshi aliamuru askari wake kumfungua vifungo Paulo"

Akamleta Paulo chini

Kutoka kwenye ngome, kuna njia ya kutelemka chini mpaka kwenye uwanda wa nje wa hekalu"

Acts 23

Matendo 23 Maelezo kwa Jumla

Muundo na Mpangilio

Tafsiri zingine zinanukuu kutoka Agano la Kale kwenye kulia kwa ukurasa kuliko maandiko yote kwa jumla. ULB hufanya hivi kupitia kilichonukuliwa katika 23:5

Dhana maalum katika sura hii

Ufufuko wa wafu

Wafarisayo waliamini kwamba baada ya watu kufa, wangefufuka tena na Mungu awazawadie ama awaadhibu. Wasadukayo waliamini kwamba pindi watu wanapokufa,hawangefufuka. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#raise and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#reward)

"Waliita laana"

Wayahudi wengine waliahidi Mungu kutokula ama kunywa mpaka Paulo auliwe na wakamuomba Mungu awaadhibu kama hawangetekeleza ahadi yao.

Uraia wa Urumi

Warumi walidhani Kwmaba ni Warumi pekee yao waliostahili kuhudumiwa kwa haki. Wangewatenda watakavyo wale ambao hawakuwa raia wa Urumi lakini kwa Warumi waliwatendea kufuata sheria. Watu wamojf walizaliwa raia wa Roma na wengine wakalipa pesa serikali ya Warumi ili wawe raia. "Kiranja Mkuu" angeadhibiwa kwa kuwatendea raia wa Urumi sawa wale wasiokuwa raia.

Mifano ya usemi muhimu katika sura hii

Chokaa

Hii ni mfano ya kawaida katika Maandiko matakatifu inayoonyesha mtu kuwa mzuri au kitu kuwa kizuri na safi ama mwenye haki lakini yule mtu ni mwovu ama amejinajisi ama si wa haki.

<< | >>

Acts 23:1

Sentensi unganishi

Paulo anasimama mbele ya wakuu wa makuhani na wajumbe wa baraza.

Ndugu zangu

Hii ina maana " Wayahudi."

Nimeishi mbele za Mungu na dhamiri njema mpaka leo

"Mimi najua kuwa hata leo nimefanya kila kitu Mungu alichotaka mimi kufanya"

Anania

Ni mtu tofauti na Anania anayetajwa sura ya 5:3

ukuta uliopakwa chokaa

Inamaanisha ukuta uliopakwa chokaa ili uonekane kuwa safi. Paulo anamwambia Anania kuwa anaonekana safi kama ukuta uliopakwa chokaa lakini ndani kumejaa uovu.

Umeketi kuhukumu ... kinyume cha sheria?

Paulo anatumia swali ili kumdhihirisha Anania kuwa ni mnafiki.

Acts 23:4

Je, hii ni jinsi unavyo mtukana kuhani mkuu wa Mungu?

wanaume walitumia swali hili kumkemea Paul kwa nini alisema. "Usimtusi Kuhani Mkuu wa Mungu!

Kwa maana imeandikwa

Paul ananukuu mambo ambayo Musa aliandika katika sheria. Hii inaweza kuwa: "Kwa maana Musa aliandika katika sheria"

Acts 23:6

Ndugu zangu

Hapa "Ndugu zangu" maana yake "Wayahudi wenzake"

mwana wa Mfarisayo

Hapa "mwana" maana yake yeye ni mwana halisi wa Farisayo na pia mtoto wa farisayo. "baba na mababa zake walikuwa mafarisayo"

Kwa ujasiri nakubali ufufuo wa wafu

neno "ufufuo" linaweza kumaanisha "kurudi kwenye maisha." kivumishi cha jina "wafu" inaweza kuwa "wale waliokufa." "Mimi kwa ujasiri nakubali wale waliokufa watarejea katika maisha"

Nimekwisha kuhukumiwa

"Mnanihukumu juu ya jambo hili"

mkutano ukagawanyika

"watu katika umati kwa nguvu hawakukubaliana wao kwa wao"

Kwa maana Masadukayo ... lakini Mafarisayo

Hii ni taarifa za msingi kuhusu Masadukayo na Mafarisayo.

Acts 23:9

Hivyo ghasia kubwa ikatokea

"Walianza kupiga kelele kwa sauti kubwa miongoni mwao." neno "hivyo" inaelezea tukio lililotokea kwa sababu ya kitu kingine kilichotokea hapo awali. Katika kesi hiyo, tukio liliopita ni la Paulo kuzungumzia imani yake juu ya ufufuo.

Vipi kama roho au malaika ameongea na yeye?

Mafarisayo wanawakemea Masadukayo na kudhibitisha kwamba roho na malaika wapo na wanaweza kuzungumza na watu. "Labda roho au malaika amesema naye!"

Wakati mabishano makali yalipotokea

Neno "mabishano makali" linaweza kuwa "Mwanzo wa vurugu"

Jemedari wa kikosi

Afisa wa jeshi la Kirumi au kiongozi wa askari wapatao 600.

Paulo angegawanywa vipande viwili na wao

Inamaanisha Paulo angeweza kuraruliwa vipande na kusababusha maumivu ya mwili.

kumchukua kwa nguvu

"kutumia nguvu za kimwili kumwondoa mahali pale"

ndani ya ngome

Ngome ilikuwa imeunganika na uwanda wa nje wa hekalu.

Acts 23:11

Usiku uliofuata

Hii ina maana usiku baada ya siku Paulo alipokwenda mbele ya Baraza. "Usiku huo"

utashuhudia katika Roma

maneno "kuhusu mimi" yameeleweka. "kutoa ushuhuda juu yangu katika Roma" au "kutoa ushuhuda juu yangu katika Roma"

Acts 23:12

Sentensi unganishi

Wakati Paulo akiwa kifungoni kwenye ngome, Wayahudi wasioamini waliapa kumwua.

Azimio

"kufanya nadhiri" au "kuapa mbele za Mungu"

Azimio

Ni makubaliano ya kawaida ya kufanya jambo fulani.

kuita laana juu yao wenyewe

Neno "laana" Walimwomba Mungu awalaani hama wasingetimiza nadhili yao

wanaume arobaini

wanaume 40

ambao walifanya njama hii

"ambao alipanga kumuua Paulo"

Acts 23:14

Tumejiweka wenyewe chini ya laana kubwa, kutokula kitu chochote hata tumwue Paulo

kuapa na kumwomba Mungu ili awalaani kama hawatatimiza nadhiri zao ni kusema kana kwamba laana ilikuwa kitu walichokibeba juu ya mabega yao. Sisi tumeapa tusile chochote hata tumwue Paulo na tumemwomba Mungu pia atulaani kama hatuwezi kufanya kile tulicho ahidi kufanya"

Sasa

Hii haina maana "wakati huu," lakini imetumika kuweka umakini kwa hatua muhimu ifuatayo.

Kwahiyo

Neno 'kwahiyo" linaonyesha kuna ujumbe uliotangulia kusemwa awali.

mlete chini mbele yako

"Mlete Paulo kutoka ngomeni ili akutane nawe hapa"

kana kwamba mnaamua kesi yake kwa usahihi

"kana kwamba mnataka kujifunza zaidi juu ya kile Paulo amekifanya"

Acts 23:16

kulikuwa na njama

"walikuwa tayari kwa kumshambulia Paulo" au "walikuwa wakisubiri kumwua Paulo"

ngome

Ngome ilikuwa imeunganishwa na uwanda wa nje wa hekalu.

Acts 23:18

Paulo yule mfungwa aliniita akataka nikuletee

Mfungwa Paulo ameniomba kuja kuzungumza nawe.

Yule jemadari mkuu akamshika kwa mkono akajitenga naye kando

Jemedari mkuu alimshika kijana mkono na kwenda naye kando, hii inaonyesha kijana yule alikuwa mpwa wa Paulo mwenye umri wa kati ya miaka 12 hadi 15.

Acts 23:20

Wayahudi wamekubaliana

Hii haina maana Wayahudi wote. "Baadhi ya Wayahudi wamepatana"

kumleta Paulo chini

"kumleta Paul chini kutoka kwenye ngome"

walikuwa wanakwenda kumwuliza kwa usahihi kuhusu kesi yake

"wanataka kujifunza zaidi juu ya nini Paulo amefanya"

wanaume arobaini

"wanaume 40"

Wamejificha wanamsubiri

"tayari kumwotea Paulo" au tayari kumwua Paulo"

Wameita laana ishuke chini yao wenyewe, kwa kutokula wala kunywa mpaka watakapokuwa wamemwua

"Wao walikuwa wameapa kutokula wala kunywa chochote mpaka wamemwua Paulo. Na kumwambia Mungu awalaani kama hawatafanya walichoahidi kufanya"

Acts 23:22

Taarifa ya jumla

Felix aliyekuwa mkazi wa Kaisaria alikuwa ni Gavana wa sehemu ya Rumi

aliwaita kwake

"aliwaita yeye mwenyewe"

maakida wawili

Maakida wake wawili

wapanda farasi sabini

"Wapanda farasi 70"

askari mia mbili wa mikuki

"Askari 200 ambao wanajilinda kwa mikuki"

saa tatu usiku

Hii ilikuwa yapata 9:00 usiku.

Acts 23:25

Taarifa ya jumla

Jemedari mkuu anaandika barua kwa Gavana Feliki kuhusu kukamatwa kwa Paulo.

Klaudio Lisia kwa Gavana mheshimiwa Felix, salamu

Hii ni njia rasmi ya mwanzo wa barua. Mkuu wa jeshi akimaanisha mwenyewe katika nafsi ya tatu. Nina andika kwa Klaudio Lisia, wewe mheshimiwa Liwali Feliki salamu kwako"

Mheshimiwa Gavana Felix

Feliki alikuwa mtawala wa Kirumi aliyejitakia heshima kuu

Mtu huyu alikamatwa na Wayahudi

Hapa "Wayahudi" maana yake "baadhi ya Wayahudi." Hii inaweza ikasemwa: "Baadhi ya Wayahudi walimtia mbaroni mtu huyo"

alikuwa karibu kuuawa

"walikuwa tayari kumwua Paulo

nikaenda pamoja na kikosi cha askari

Nilikuwa pamoja na maaskari wangu pale Paulo alipokuwa pamoja na Wayahudi

Acts 23:28

Nilitaka kujua neno

"mimi" inahusu Klaudio Lisia.

alikuwa ameshitakiwa kwa ajili ya maswali ya sheria yao

Walikuwa wakumtuhumu kwa kumwuliza maswali.

lakini kwamba kulikuwa hakuna tuhuma ambayo ingehitaji mauti ama kifungo.

Maneno "mauti" au "kifungo" yanaweza kuwa; hakukuwa na kitu kinyume cha mamlaka ya Kirumi cha kumwua ama kumtupa gerezani.

Kisha ikajulikana kwangu

"Baadaye nilikuja kubaini"

Acts 23:31

Basi, askari walitii maagizo yao

neno "hivyo" linaweka alama kuwa tukio hilo lilitokea kwasababu ya kitu kingine kilichotokea hapo awali. Katika kesi hiyo, tukio lililopita ni mkuu wa jeshi kuamuru maaskari kumsindikiza Paulo.

walichukua Paul na wakampeleka usiku

Hapa "kuleta" inaweza kutafsiriwa kama "chukua". "walimpata Paulo na kumpeleka wakati wa usiku"

Acts 23:34

aliuliza mkoa gani Paulo alikotokea

"Alimwuliza Paulo mkoa gani aliotokea?"

Alipojua kwamba alikuwa ametoka mkoa wa Kilikia, alisema

"wakati liwali alipotambua kuwa Paulo alikuwa ametoka mkoa wa Kilikia, liwali alisema." Hii yaweza tajwa kama nukuu ya moja kwa moja. "Paulo alisema, 'Mimi nimetokea Kilikia.' Kisha liwali akasema"

Nitasikia kutoka kwako kikamilifu

"Nitakusikiliza kwa yale yote utakayo yasema"

akaamuru awekwe

Hii inaweza ikasemwa: "akaamuru askari amweke Paulo" au "akamwamuru askari amtunze Paulo"

Acts 24

Matendo 24 Maelezo kwa jumla

Muundo na Mpangilio

Paulo alimwambia mkuu wa mkoa kwamba hakutenda tukio aliloshtakiwa na Wayahudi na kwa hivyo asimwadhibu kwa asilotenda.

Dhana maalum katika sura hii

Heshima

Viongozi wote Wayahudi (Matendo 24:2-4) na Paulo walianza kutoa hotuba zao wakitumia maneno yakudhihirisha heshima kwa mkuu wa mkoa.

Matatizo mengine katika hii tafsiri

Viongozi wa Kiserikali

Maneno "mkuu wa mkoa", Kamanda," na "akida" yanaweza kuwa magumu kutafsiri katika lugha nyingine.

<< | >>

Acts 24:1

Sentensi unganishi

Paulo sasa yuko kwenye misukosuko. Tertulo anawasilisha mashitaka kwa Liwali Feliki dhidi ya Paul.

Baada ya siku tano

"Siku tano baada ya askari wa Kirumi kumchukua Paul kwenda Kaisaria"

Anania

Angalia jinsi gani unaweza kulitafasiri katika 23:1

msemaji

"mwanasheria." Tertulo alikuwa mtaalam wa sheria ya Kirumi. Alikuwa huko kumshtaki Paul mahakamani.

Tertulo

Hili ni jina la mtu mwanamume.

walikwenda huko

"alienda Kaisaria ambako Paulo alikuwa"

alisimama mbele ya Gavana

"mbele ya Gavana ambaye alikuwa jaji wa mahakama"

akaanza kumshtaki

"alianza kuleta ukiukwaji wa sheria ya Kirumi dhidi yake"

tuna amani kubwa

"sisi, raia tulio chini ya utawala wa Felix tuna amani kubwa"

na kwa maono yako yanaleta mageuzi mazuri katika taifa letu

"na kupitia mipango yako mizuri imeleta mabadiliko makubwa katika taifa letu"

Feliki

Angalia jinsi gani unaweza kuitafasili katika

na mtizamo wako huleta mageuzi nzuri kwa taifa letu

"na mipango yako imeboresha sana taifa letu"

Mweshimiwa Felix

Angalia jinsi gani unaweza kuitafasili katika 23:25

Acts 24:4

Taarifa ya jumla

Fungu hili linazungumzia juu ya Anania, baadhi ya wazee na Tetulo

Lakini nisikuchoshe zaidi

Maana inawezekana ni 1) "ili mimi nisichukue sana muda wako" au 2) "Hivyo kwamba nisikufunge."

kwa wema waka nisikilize kwa ufupi

"kusikiliza hotuba yangu fupi"

Tumegundua kwamba mtu huyu mkorofi

neno "sisi" inamaanisha Anania, wazee kadhaa na Tertulo. "sisi tulimshuhudia Paulo" au "tuligundua kwamba Paulo chazo cha matatizo"

Wayahudi wote kila mahali duniani

neno "wote" hapa ni kuongezewa chumvi kama kisingizio cha kumshtaki Paulo. "Wayahudi wote duniani kote"

Tena ni kiongozi wa madhehebu ya Wanazorayo

Neno "dhehebu la Wanazarayo" ni jina jingine kwa wakristo "Mtu huyu anaongoza makundi ya watu wafuasi wa madhehebu ya Wanazarayo""

dhehebu

hili ni kundi dogo ya watu ndani ya kundi kubwa. Tertulo anaona Wakristo kuwa kundi dogo ndani ya Uyahudi.

Acts 24:7

Sentensi unganishi

Tertulo anamaliza kuwasilisha mashtaka ya Paulo kwa Gavana Feliki.

anamshitaki

"kumshtaki Paulo kwa kufanya" au "kumshtaki Paulo kwa kuwa na hatia ya kufanya"

Wayahudi

Hii inamaana ya viongozi wa Wayahudi waliokuwa pale katika kesi ya Paulo.

Acts 24:10

Sentensi unganishi

Paul anaitikia kwa Gavana Feliki kuhusu mashtaka yaliyowasilishwa dhidi yake.

Gavana alimwashiria

"gavana akitoa ishara"

mwamuzi wa taifa hili

Neno "taifa" linamaanisha watu wa taifa la Kiyahudi. "Mwamuzi wa wa watu wa taifa la Wayahudi"

Kujieleza mwenyewe

"Kuielezea hali yangu"

waweza kuhakikisha

"unauwezo wa kufuatilia na kuthibitisha"

siku kumi na mbili tangu

"Siku 12 tangu"

sikuweza kuhamasisha kusanyiko"

Neno "kuhamasisha" ni kuwafanya watu wasiwe na utulivu"

mashitaka

"Lawama juu ya matendo maovu" au "mashitaka ya uharifu"

Acts 24:14

Nakiri hili kwenu

"Mimi nakiri hili kwako" au "ninatubu hili kwako"

wanaita dini

"wanaita kundi la wazushi"

kwa namna ile namtumikia Mungu wa babu zetu

Hii inamaana kwamba Paulo anadai kufuata dini ya kale, ambayo kwa ufafanuzi si dini mpya, "madhehebu."

kama watu hawa

Hapa "watu hawa" inahusu Wayahudi ambao ndio wanamtuhumu Paulo mahakamani.

ufufuo ujao wa wafu....kwa wote wenye haki na wasio na haki.

neno "ufufuo" linaweza kutumika kama "Kurudishwa katika maisha na Mungu." Na, neno "wafu" linaweza kuwa "wale waliokufa." "wakati Mungu akiwarudisha katika uhai wale wote waliokuwa wamekufa"

wasio wa haki

"wale waliofanya mambo mabaya"

Nafanya kazi

"Nafanyakazi vizuri"

kuwa na dhamiri bila lawama

Hapa "dhamiri" inahusu maadili ndani ya mtu kuwa akiamua kati ya mema na mabaya. "kuwa bila lawama" au "daima kutenda haki"

mbele za Mungu

"Katika uwepo wa Mungu"

Acts 24:17

Sasa

neno hili linaweka alama ya kuhama kutoka katika hoja ya Paulo. Hapa anaanza kuelezea hali katika Yerusalemu wakati baadhi ya Wayahudi walipomweka Paulo nguvuni.

baada ya miaka mingi

"baada ya miaka mingi kutoka Yerusalemu"

Nilikuja kuleta misaada kwa taifa langu na zawadi ya fedha

Hapa "nilikuja" inaweza kutafsiriwa kama "Nilikwenda." "Nilikwenda kusaidia watu wangu kwa kuwapelekea fedha kama zawadi"

katika sherehe ya utakaso katika hekalu

"katika hekalu baada ya kumaliza sherehe ya kujitakasa mwenyewe"

Bila umati wa watu au ghasia

Hii yaweza tajwa kama kauli mpya. "Mimi nilikuwa sijakusanya umati wala sikujaribu kuanzisha ghasia"

wamaume hawa

"Wayahudi kutoka Asia"

kama wanajambo lolote

"Kama wana jambo lolote la kusema"

Acts 24:20

Sentensi unganishi

Paul alimaliza kumjibu Gavana Feliki kuhusu mashtaka yaliyowasilishwa dhidi yake.

wanaume hawahawa

Hii ina maana ya wajumbe wa baraza ambao walikuwepo Kaisaria katika kesi ya Paulo.

lazima waseme kosa waliloliona kwangu

"waseme iwapo kuna kitu kibaya nilikifanya na kukithibitisha"

Ni kuhusu ufufuo wa wafu

neno "ufufuo" linaweza kutumika kama "Kurudishwa katika maisha na Mungu." Na, neno "wafu" linaweza kuwa "wale waliokufa." "wakati Mungu akiwarudisha katika uhai wale wote waliokuwa wamekufa"

Ninahukumiwa leo na wewe

hii inaweza semwa kama "mnanihukumu mimi leo hii"

Acts 24:22

Taarifa ya jumla

Felix alikuwa Gavana wa Kirumi katika eneo la mji wa Kaisaria.

Njia

Hili lilijuwa jina jingine la ukristo.

Wakati wowote Lisia mkuu wa kikosi anakuja hapa chini

"wakati Lisia mkuu wa kikosi anakuja chini" au "muda Lisia mkuu wa kikosi anakuja chini"

Mimi nitaamua kesi yenu

"Nitafanya uamuzi kuhusu shutuma hizo dhidi yako" au "nitatoa hukumu kama wewe una hatia"

awe na uhuru

"Paulo anapewa uhuru si vinginevyo ni miongoni mwa wafungwa"

Acts 24:24

Baada ya siku kadhaa

"Baada ya siku kadhaa"

Drusila mkewe

Drusila ni jina la mwanamke.

Myahudi

Hii ina maana Myahudi wa kike. "ambaye alikuwa Myahudi"

Felix akajawa na woga

Felix inaweza kuwa aliona uthibitisho wa dhambi zake.

kwa sasa

"kwa wakati huu wa sasa"

Acts 24:26

Paulo angempa fedha

Feliki alikuwa na matumaini Paul atatoa rushwa ili amwachie huru.

hivyo mara nyingi alimwagizia na kuongea naye

"hivyo Feliki mara nyingi alimwagizia Paulo aletwe azungumza naye"

Porkio Festo

Huyu alikua Gavana mpya wa Rumi aliyechukua nafasi ya Feliki.

alitaka kujipendekeza kwa Wayahudi

Hapa "Wayahudi" inamaanisha viongozi wa Wayahudi. "alitaka viongozi wa Wayahudi wampende"

alimwacha Paulo aendelee kuwa chini ya ulinzi

"alimwacha Paulo gerezani"

Acts 25

Matendo 25 Maelezo kwa jumla

Dhana maalum katika sura hii

Neema/Msaada maalum

Neno hili limetumika kwa njia mbili katika sura hii. Wakati viongozi Wa Wayahudi walipomwomba Festus neema, walikuwa wanamuomba kuwafanyia kitu maalum ambacho hajazoea kukifanya. Wakati Festus "alitaka kupata neema ya Wayahudi", alitaka wakuwe kama yeye na wakuwe" tayari kumtii miezi na miaka inayokuja. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#favor)

Uraia wa Urumi

Warumi walidhani kwamba ni Warumi pekee yao waliostahili kuhudumiwa kwa haki. Wangewatenda watakavyo wale ambao hawakuwa raia wa Urumi lakini kwa Warumi waliwatendea kufuata sheria. Watu wamoja walizaliwa raia wa Roma na wengine wakalipa pesa serikali ya Warumi ili wawe raia. Wafanyakazi wa serikali wangeadhibiwa kwa kuwatendea raia wa Urumi sawa na wale wasiokuwa raia.

<< | >>

Acts 25:1

Taarifa kwa ujumla

Festo ndiye gavana wa Kaisaria

Sasa

Neno hili linaonyesha mwanzo wa tukio linalofuata kwenye simulizi.

Festo akaingia katika jimbo

Inamaanisha 1) Festo aliingia katika eneo au 2) Festo aliingia kwenye eneo ili kuanza kutawala

Alienda toka Kaisaria mpaka Yerusalemu

Hii inamaanisha 1) kwenda juuinaonesha umuhimu wa Yerusalemu au 2) alikwenda mpaka juu kwa kuwa Yerusalemu ipo kilimani.

Walileta mashitaka dhidi ya Paulo

"kumshtaki Paulo kwa kuvunja sheria"

Waliongea kwa nguvu kwa Festo

"walimbembeleza Festo"

Kwamba atamuita..... ili wamuue

"kwamba Festo atamuita Paulo..... ili Wayahudi wamuue"

Anaweza kumuita

Anaweza kumtuma

Wanaweza kumuua njiani

Watamvamia Paulo na kumuua akiwa njiani

Acts 25:4

Paulo alikuwa mfungwa Kaisaria

Paulo ni mfungwa Kaisaria na mimi mwenyewe ntarejea huko baada ya muda mfupi.

Kama kuna jambo lolote baya kwa mtu huyu.

Kama Paulo amefanya jambo lolte baya.

Unaweza kumshtaki

"Unaweza kuleta mashtaka" au "unaweza kumshataki kwa kuvunja sheria"

Acts 25:6

Baada ya kukaa

Baada ya Festo kukaa

Kukaa kwenye kiti cha hukumu

" kukaa juu ya kiti ili afanye kazi ya hakimu"

Paulo aletwe kwake

"kwamba wamlete Paulo kwake"

Alipofika

"Paulo alipofika na kusimama mbele ya Festo"

Jina la Wayahudi

"sheria ya wayahudi"

siyo dhidi ya hekalu

Paulo alisema hajavunja sheria yoyote kuhusu nani aingie kwenye hekalu la Yerusalemu. "siyo dhidi ya sheria za kuingia hekalini"

Acts 25:9

Alitaka kujipendekeza kwa Wayahudi

Alitaka kuwaridhisha wayahudi

Na kuhukumiwa na mimi juu ya mambo haya huko

"Ntakapokuhukumu kutokana na mashitaka haya"

Sehemu ninayopaswa kuhukumiwa

"Ni sehemu gani ambapo wewe itanihukumu"

Acts 25:11

Maelezo yanayounganisha

Paulo akaendelea kuongea na Festo

Ikiwa nimefanya kinachostahili kifo

"ikiwa nimefanya jambo baya la kustahili adhabu ya kifo"

Ikiwa mashitaka si kitu

"ikiwa mashitaka yao juu yangu si ya kweli"

Hakuna anayeweza kunikabidhi kwao

Hii inamaanisha 1) Festo hana mamlaka ya kisheria ya kumkabidhi Pailo kwa waliomshaki mashitaka ya uongo au 2) Paulo alisema kwamba kama hajafanya kosa lolote basi gavana asisikilize maombi ya Wayahudi.

Namuomba Kaisari

"Naomba kwamba niende mbele ya Kaisari ili nisikilizwe"

Festo aliongea na baraza

Hili ni baraza la kisiasa la serikali ya Roma. "Festo aliongea na washauri wa serikali yake"

Acts 25:13

Maelezo ya jumla

Festo akaanza kuelezea kesi ya Paulo kwa mfalme Agripa.

Sasa

Neno hili linaonyesha mwanzo wa tukio jipya kwenye simulizi.

Mfalme Agripa na Bernike

Agripa alikua mfalme aliyetawala wakati huo na Bernike alikuwa dada yake.

Kumtembelea kiofisi

"kumtembelea Festo kuhusu masuala ya kiofisi.

Mtu mmoja aliachwa na Felix kama mfungwa.

Wakati Felix akiacha ofisi alimuacha mtu gerezani.

Acts 25:17

Kwa hiyo

Neno hili linanyesha maelezo ya kilichosemwa kabla. Hivyo Festo alisema mtu aliyeshitakiwa anatakiwa awakabili washitaki wake na kujitetea.

Walipokuja pamoja hapa

"wakati viongozi wa Kiyahudi walipokuja kuonana na mimi hapa"

Nilikaa kwenye kiti cha hukumu

"Nilikaa juu ya kiti ambacho nilifanya kazi ya hakimu"

Niliamuru mtu huyo aletwe ndani

"Niliamuru askari wamlete Paulo mbele yangu"

Dini yao wenyewe

Neno "dini" linamaanisha mfumo wa imani ya watu juu ya maisha na nguvu.

Kuhukumiwa kule juu ya mambo haya

"ambapo baraza la Wayahudi wataamua kama anamakosa kuhusu masitaka haya"

Acts 25:21

Maelezo yanayounganisha

Festo akamaliza kuelezea kesi ya Paulo kwa mfalme Agripa

Niliamuru awekwe

"Niliwaambia maaskari wamuweke garezani"

"Keso" Festo akasema "utamsikia"

"Festo akasema, 'ntapanga ili usikilize Paulo kesho"

Acts 25:23

Paulo aliletwa kwao

"Walimpeleka Paulo mbele zao"

walinipigia kelele

"Wayahudi waliongea na mimi kwa nguvu"

Asiendelee kuishi

Maelezo haya yanaweka mkazo wa kinyume cha kusema "afe maramoja"

Acts 25:25

Maelezo yanayounganisha

Festo akaendelea kuongea na Mfalme Agripa

Nimemleta kwenu, hasa kwako, Mfamle Agripa

" Nimemleta Paulo kwenu nyote lakini hasa kwako Mfalme Agripa"

Ili nipate cha kuandika zaidi

"ili nipate cha ziada cha kuandika" au "ili nijue niandike nini"

haina maana kumpeleka mfungwa na bila kuonyesha mashitaka yanayomkabili

"itakuwa na maana nikimpeleka mfungwa na kuonyesha mashtaka yanayomkabili"

Mashitaka dhidi yake

inamaanisha kuwa 1) mashitaka yaliyoletwa juu yake na viongozi wa Kiyahudi au 2) mashitaka chini ya sheria za Roma yanayoelezea kesi ya Paulo.

Acts 26

Matendo 26 Maelezo kwa jumla

Muundo na Mpangilio

Hii ni mara ya tatu kwa kusema habari ya kubadilishwa kwa Paulo. Hii ni kwa sababu hili ni tukio muhimu kwenye Kanisa la awali. Kuna mara tatu ya kusema kubadilishwa kwa Paulo. (Tazama: Matendo 9 na 22)

Paulo alimwelezea Mfalme Agripa kwa nini alikitenda alichokitenda na ya kwamba mkuu wa mkoa asimuadhibu kwa hicho.

Dhana Maalum katika sura hii

Mwanga na giza

Kila mara Biblia huzungumzia watu wasiokuwa waadilifu, watu wasiotenda yanayompendeza Mungu kana kwamba wanatembea gizani. Inazungumzia mwanga kama kinachowawezesha wenye dhambi kuwa waadilifu baada ya kugundua kwamba wanachofanya si kizuri na kumheshimu Mungu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous)

<< | >>

Acts 26:1

Maelezo anayounganisha

Festo alimpeleka Paulo mbele ya Mfalme Agripa. Kwenye mstari wa pili Paulo anaanza kutoa utetezi wake kwa Mfalme Agripa.

Alinyoosha mkono wake

"ilinyoosha mkono wake mbele ya makutano ili apate umakini wao"

Akaweka utetezi wake

Akaakza kujitetea mwenyewe dhidi ya mashitaka"

ninajina mwenye furaha

Paulo alikuwa na furaha akatumia kuwepo kwake mbele ya Agripa kama nafasi ya kuongea juu ya injili.

Acts 26:4

Wayahudi wote

Inamaniisha 1)Mafarisayo walikua na Paulo na walimfahamu kama Mfarisayo au 2)"Paulo alijulikana sana kwa Wayahudi

Kwenye nchi yangu mwenyewe

Ina maanisha 1) kwa watu wake mwenyewe sio lazima wawe kwenye eneo la Israeli au 2) kwenye ardhi ya Israeli.

Acts 26:6

Sasa

Paulo alitumia maneno haya kuonesha utetezi mwingine.

Nimesimama hapa ili nihukumiwe

"Nipo hapa waliponiweka ili nihukumiwe"

Naziangalia ahadi ambazo Mungu aliwapa baba zetu

Paulo ana matumaini na kuja kwa Mesia.

Nategemea kuifikia

"Tunaamini kuwa tutapokea ahadi ambayo Mungu ametuahidi"

Kwa nini mnafikiri ni ajabu kwa Mungu kufufua wafu?

Paulo alisema haya ili kumfanya Agripa aunganishe aliyoyasema Paulo na ambacho Agripa alikiamini juu ya Mungu anavyoweza kufufua wafu. "Wewe mwenyewe unaamini kuwa Mungu anaweza kufufua wafu"

Acts 26:9

Wakati fulani

Paulo alitumia maneno haya kuonesha utetezzi wake mwingine. Sasa anaelezea alivyokuwa anawatesa watakatifu.

Kinyume na jina la Yesu

neno "jina" linasimama kwa ujumbe wa Yesu. "kinyume na ujumbe wa Yesu"

Nipe kura yangu dhidi yao

"Kupiga kura ili kuwaadhibu"

Niliwaadhibu mara kwa mara

Inamaanisha 1)Paulo aliwaadhibu baadhi ya waamini mara nyingi au 2) Paulo aliwaadhibu waamini mbalimbali.

Acts 26:12

Nilipokuwa nafanya hivi

Paulo alitumia maneno haya kuonesha ushahidi mwingine. sasa anaelezea namna Yesu alipomuita toka kwenye kuwatesa watakatifu na kumfuata yeye.

Nilipokuwa

neno hili limetumika kuonesha matukio mawili yanayotokea kwa wakati mmoja. Hapa Paulo alikuwa anawatesa watakatifu alipokuwa akienda Dameski.

Kwa mamlaka na maagizo

Paulo alikuwa na barua toka kwa viongozi wa kiyahudi wakimpa mamlaka ya kuwatesa waamini wa Kiyahudi.

Ni vigumu kwako kuupiga teke mchokoo

Mungu anafananisha kukataa kwa Paulo kuhusu mipango ya Mungu na ng'ombe anayepiga teke fimbo ya mkulima. "ngumu kwako kupambana na maelekezo ya Mungu kwako."

Acts 26:15

Maelezo yanayounganisha

Paulo aliendelea kutoa utetezi wake kwa Mfalme Agripa. Kwenye mistari hii aliendelea kunukuu mazungumzo yake na Bwana.

Nilijitenga mwenyewe

"Nilitengezeza mwenyewe" au "Kuweka wakfu mwenyewe"

kwa imani iliyo kwangu

Hii inaelezea Imani juu ya Mungu kwa waliotengwa na Mungu kwa ajili yake.

Niliowatenga kwa ajili yangu kwa imani iliyo kwangu

Paulo alimaliza kumnukuu Bwana

Acts 26:19

Kwa hiyo

Neno hili linanyesha maelezo ya kilichosemwa kabla. Paulo alielezea ambacho Bwana alimuamuru katika maono.

Sikuyapuuza maono ya mbinguni

"Nilitii ujumbe niliopewa kwenye maono yaliyotoka mbinguni"

Acts 26:22

Maelezo yanayounganisha

Paulo akamaliza kujitetea kwa Mfalme Agripa

Ambayo manabii

Paulo anamanisha maandishi yaliyokusanywa ya Manabii wa Agano la kale.

Kwamba Kristo atateseka

"Kwamba kristo atateseka na kufa"

kutangaza mwanga

Kutangaza ujumbe wa ukombozi"

Acts 26:24

Una wendawazimu

"Unaongea upuuz"i au "umechanganyikiwa"

Mimi sio mwendawazimu

"Mimi ni mzima" au "nina uwezo wa kufikiri vizuri"

Mtupu

"uzito" au "kuhusu jambo lenye uzito"

Naongea kwa uhuru kwake

Naongea kwa uhuru kwa Mfalme Agripa

Haikufanywa kwenye kona

"Haikufanywa kwa siri"

Acts 26:27

Unawaamini managii, Mfalme Agripa?

Paulo alimuuliza swali hili Agripa na Agripa alishaamini waliyosema manabii kuhusu Yesu. "umeshaamini waliyosema manabii wa Kiyahudi Mfalme Agripa!"

Kwa mda mfupi unaweza kunishawishi na kunifanya niwe Mkristo?

Agripa aliuliza hili swali ili kumuonyesha Paulo kwamba haawezi kumshawishi Agripa kirahisi bila kithibitisho. "Unafikiri unaweza kunishawishi kirahisi!"

Acts 26:30

Ndipo Mfalme akasimama na Gavana

Kisha Mfalme Agripa akasemama pamoja na Gavana Festo"

Acts 27

Matendo 27 Maelezo ya jumla

Dhana muhimu katika sura hii

Kusafiri Majini

Watu walioishi karibu na bahari walisafiri kutumia boti zilizosukumwa na upepo. Wakati wa kipindi fulani mwakani, upepo ungeelekea mwelekeo usiyofaa hadi ikawa vigumu sana kusafiri majini.

Uaminifu

Paulo alimwamini Mungu kama atamwezesha kusafiri kwa usalam hadi atakapofika inchi kavu. Aliwaambia mabaharia na wanajeshi kuamini pia kwamba Mungu atachunga maisha yao. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#trust)

Paulo anaumega mkate

Luka anatumia maneno karibu kuwa sawa na yale aliyotumia kueleza habari ya karama mwisho wa Yesu pamoja na wanafunzi wake. Alichukua mkate, akashukuru Mungu na kuumega na kula. Hata hivyo tafsiri yako isimfanye msomaji kufikiria kwamba Paulo alikuwa anaongoza sherehe ya kidini.

<< | >>

Acts 27:1

Sentensi unganishi

Paulo, kama mfungwa , anaanza safari kwenda Rumi

Taarifa

Neno sisi linamaanisha Luka mwandishi pamoja na Paulo na wasafiri wengine waliosafiri na Paulo

Taarifa

Adramitamu ni mji uliokuwa pwani ya uturuki ya sasa

Wakawaeka Paulo na wafungwa wengine chini ya mashitaka ya Julio wa kikosi cha Agustani

Maaskari wa kirumi wakamweka kwa afisa Julias wa Agustani kwa mkuu wa Paulo na wafungwa wengine.

Acts 27:3

Taarifa kwa ujumla

Neno sisi linamaanisha Luka, Paulo na wote waliosafiri pamoja naye.

Juliasi alimtendea Paulo kwa ukarimu

Julias alimtendea vizuri Paulo

Akasafiri kuzunguka kisiwa cha Kipro ambacho kilikuwa kimeukinga upepo.

Neno Kukinga linaweza kusemwa katika hali tendaji.

Acts 27:7

Tuliposafiri pole pole mwishowe tulifika kwa taabu.

Unaweza kuonesha kuwa kilichofanya wakasafiri kwa taabu ilikuwa ni kwa sababu ya upepo ulivuma dhidi yao.

Karibu na mji wa Lasi

Huu ni mji katika Pwani ya Krete

Acts 27:9

Taarifa kwa ujumla

Maneno kama "sisi" "Tuli" inamaanisha Paulo na wengine waliokuwa katika meli.

Muda wa mfungo wa wayahudi ulikuwa umepita na haikuwa sasa hatari kusafiri.

Mfungo huu ulifanyika katika siku ya utakaso ambayo mara nyingi ilifanyika mwishoni mwa mwezi wa septemba au mwanzoni mwa mwezi wa octoba katika kalenda ya watu wa magharigi. Baada ya muda huo ilikuwa hatari kutokana na vimbunga vya mara kwa mara.

Acts 27:12

Bandari haikuwa sehemu rahisi kukaa wakati wa baridi.

Unaweza kuonesha kwa nini haikuwa rahisi kukaa bandarini. "Bandari haikuweza kutosheleza kuleta usalama kwenye gati za meli wakati wa baridi na vimbunga"

Kaskazini mashariki na Kusini mashariki

Pande hizi hutegemea mahali jua linako chomozea na mahali jua linapozamia. Kaskazini Mashariki inaweza kuwa kushoto kiasi mwa upande unao chomoza jua. Kusini mashariki inakuwa ni kulia kiasi mwa upande wa jua linako zamia.

Acts 27:14

Wakati meli ilipolemewa na kushindwa kuukabili upepo

Upepo ulivuma kwa ukali dhidi ya upande wa kichwa cha meli kiasi kwamba hatukuweza kusafiri.

Acts 27:17

Tulipigwa kwa nguvu sana na dhoruba,

Hii inaweza kusemwa katika hali ya kutenda, Upepo ulivuma kwa nguvu"

mabaharia wakaanza kutupa mizigo kutoka Melini.

Hili lilifanyika ili kupunguza uzitoili meli isizame.

Acts 27:19

Mabaharia wakaanza kutupa vifaa kwa mikono yao wenyewe

Vifaa ina maanisha vyombo maalumu kwa ajili ya mabaharia. Hii inaonesha jinsi hali ilivyokuwa tete.

Bado dhoruba kubwa ilitupiga

Upepo wa kutisha ulitupiga sana.

Acts 27:21

Ili kupata haya madhara na hasara.

Na matokeo yake tumepata madhara na hasara.

Acts 27:23

Lazima usimame mbele ya Kaisari

Neno "Lazima usimame mbele ya Kaisari" Inamaanisha paulo kufika mbele ya mahakama na kuhukumiwa na Kaisari. "Lazima usimame mbele ya Kaisari akuhukumu"

Lakini lazima tuumie kwa kupigwa katika baadhi ya visiwa.

"Upepo lazima utatupeleka ufukweni mwa visiwa fulani."

Acts 27:27

kama usiku wa manane hivi,

Usiku wa manane unaweza kutafsiriwa kama usiku wa saa nane.

wakapata mita thelathini na sita

Mita ni kipimo kama cha urefu wa mikono.

Acts 27:30

Boti ndogo ndogo za kuokolea maisha,

Hizi ni botti au melindogo ambazo hutolewa nyuma ya meli kubwa . boti hizi huwekwa kwa ajili ya kujiokolea wakati meli inataka kuzama

Hamuwezi kuokoka isipokuwa hawa watu wanabaki kwenye meli.

Maneno ya nayayo semwa kinyume yakimaanisha hakuna uwezekano wa kuokoka mpaka watu wabaki melini.

Acts 27:33

33Wakati mwanga wa asubuhi ulipokuwa unajitokeza

Kulipokuwa kukipambazuka

Siku hii ni ya kumi na nne

Siku ya kumi na nne

Hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyenu utakaopotea

Hii ilikuwa ni njia ya usemi ulio maanisha kwamba hakuna harari yoyote ingewapata. "Kila mmoja atakuwa salama katika dhoruba hii."

Acts 27:36

wote wakatiwa moyo

Hii inaweza kusemwa katika hali tendaji, "Wote walitiwa moyo"

Tulikuwa watu 276 ndani ya meli.

Hii ni taarifa ya nyuma.

Acts 27:39

Nchi kavu majini au Ghuba

Sehemu ya nchi kavu iliyoingia majini iliyokuwa na mchanga mwing

Lakini wakaja mahali ambapo mikondo miwili ya maji inakutana,

Mkondo wa maji unaotiririka kwenda upande mmoja wakati wote. Mara nyingine zaidi ya mkondo mmoja unaweza kutiririka ukiukatisha ule mwingine. Hali hii inaweza kusababisha mchanga kulundikana mahali pamoja na kufanya kina cha maji kuwa kifupi.

Acts 27:42

Mpango wa wale askari ulikuwa

Maaskari walikuwa wanapanga

Angeogelea na kutoroka.

"Kuruka kutoka katika meli na kuingia majini"

wengine juu ya vipande vya mbao

Wengine kwenye vipande vya mbao

Acts 28

Matendo 28 Maelezo kwa jumla

Muundo na Mpangilio

Hakuna anayefahamu ni kwa nini Luka anamaliza habari hii bila kuwaambia watu kilichomtendekea Paulo baada ya yeye kuwa Roma kwa miaka miwili.

Dhana maalum katika sura hii

"Barua" na "Ndugu"

Viongozi wa Wayahudi walishangaa kwamba Paulo alitaka kuzungumza nao kwa vile hawakuwa wamepokea barua kutoka kwa kuhani mkuu Yerusalemu kusema kwamba Paulo alikuwa anakuja.

Wakati viongozi wa Wayahudi walipozungumza kuhusu "ndugu" walimaanisha Wayahudi wenzao na sio Wakristo.

Matatizo mengine ya utafsiri katika sura hii.

" Alikua mungu"

Wenyeji waliamini ya kwamba Paulo alikuwa mungu, lakini hawakuamini kwamba alikuwa Mungu wa kweli. Hatujui ni kwa nini Paulo hakuwaambia wenyeji kwamba hakuwa Mungu.

__<< | __

Acts 28:1

Sentensi unganishi:

Baada ya meli kuharibika, watu wa kisiwa cha Malta walimsaidia Paulo na wenzake waliokuwa kwenye meli. Walikaa pale miezi mitatu.

kisiwa kilichoitwa Malta

Malta ni kisiwa kilichopo katika kisiwa kingine ambacho kwa sasa kinaitwa Sisili.

watu asilia

wenyeji wa pale

Acts 28:3

shoka mkali alitokea

nyoka mwenye sumu kali alitokea kwenye mzigo wa kuni

haki pia

neno "Haki" lilimaanisha jina la Mungu waliyemwabudu.

Acts 28:5

akamkung'utia yule mnyama motoni

alitikisa mkono wake ili yule nyoka aangukie kwenye moto

walisema kuwa alikuwa mungu

labda kulikuwa na imani kwamba mtu yeyote aliyeishi baada ya kugongwa na nyoka alikuwa sio wa kawaida

Acts 28:7

Ujumbe wa jumla:

Hapa maneno "sisi" ana "sisi" yanamtaja Paulo

alifanywa kuwa mgonjwa

alikuwa mgonjwa

na liponywa

na aliwaponya wote

Acts 28:11

Sentensi unganishi:

Safari ya Paulo kwenda Rumi inaendelea

meli ya Alexandria

meli ambayo ilitoka Alexandria

ambayo ilinyauka kwenye kisiwa

wafanyakazi waliachwa kisiwani majira ya baridi

Acts 28:13

jiji la Regimu

huu ni mji wa bandari uliopo kusini magharibi mwa Italia

jiji la Puteli

Puteli kwa sasa ipo katika mji wa Napoli

Alimshukuru Mungu na kujipa moyo

hii ilimtia moyo sana

Acts 28:16

viongozi kati ya Wayahudi

hawa ni wale viongozi wa Kiyahudi au wa kidini waliopo Rumi

kinyume na watu

kinyume na Wayahudi

Acts 28:19

wayahudi

hii haimanishi Wayahudi wote bali viongozi tu

aliongea kinyume na matakwa yao

alilalamika juu ya mambo ambayo viongozi wa Kirumi walitaka kufanya

Acts 28:21

mnafikiri kuhusu dhehebu hili

dhehebu ni kundi dogo ndani ya kubwa

kwa kuwa tunaijua sisi

kwa sababu sisi tunaijua

Acts 28:23

alitenga siku kwa ajili yake

alichagua siku kwa ajili yake kuongea naye

alishuhudia kuhusu ufalme wa Mungu

ufalme wa Mungu hapa unamaanisha utawala wa Mungu kama mfalme

Acts 28:25

Sentensi unganishi:

Zviongozi wa Kiyahudi walipokuwa tayari kuondoka, Paulo alinukuu maandiko kutoka Agano la Kale kwa ajili yao

lakini hawataelewa...lakini hawatajua

Sentensi hizi mbili zinamaanisha kitu kimoja

Acts 28:27

Sentensi unganishi:

Paulo anamalizia kumnukuu nabii Isaya

na kugeuka tena

kumtii Mungu ni sawa na kumgeukia Mungu

Acts 28:28

Sentesni unganishi:

Paulo anamaliza kuongea na viongozi wa Kiyahudi

nao watasikiliza

baadhi yao watasikiliza

Acts 28:30

Sentensi unganishi:

Luka anakamilisha simulizi ya Paulo katika kitabu cha Matendo ya Mitume

alikuwa anahubiri kuhusu ufamle wa Mungu

ufalme wa Mungu una maana ya utawala wa Mungu

Utangulizi wa Warumi

Sehemu ya 1: Utangulizi wa Ujumla

Maelezo ya Kitabu cha Warumi

  1. Utangulizi (1:1-15)
  2. Uadilifu kwa imani katika Yesu Kristo (1:16-17)
  3. Watu wote wanahukumiwa kwa sababu ya dhambi (1:18-3:20)
  4. Uadilifu kupitia Yesu Kristo kwa imani kwake (3:21-4:25)
  5. Matunda ya Roho (5:1-11)
  6. Adamu na Kristo walinganishwa (5:12-21)
  7. uwa kama Kristo katika maisha haya (6:1-8:39)
  8. Mpango wa Mungu kwa Israeli (9:1-11:36)
  9. Ushauri wa manufaa kwa kuishi kama Wakristo (12:1-15:13)
  10. Hitimisho na salamu (15:14-16:27)

Nani aliandika Kitabu cha Warumi?

Mtume Paulo aliandika Kitabu cha Warumi. Paulo alitoka mji wa Tarso. Alikuwa anajulikana kama Sauli katika maisha yake ya awali. Kabla ya kuwa Mkristo, Paulo alikuwa Mfarisayo. Aliwatesa Wakristo. Baada ya kuwa Mkristo, alisafiri mara kadhaa katika Ufalme wa Roma akiwaambia watu kuhusu Yesu.

Paulo huenda aliandika barua hii alipokuwa akiishi katika mji wa Korintho wakati wa safari yake ya tatu kwenye Ufalme wa Roma.

Je, kitabu cha Warumi kinahusu nini?

Paulo aliandika barua hii kwa Wakristo huko Roma. Paulo alitaka wawe tayari kumpokea wakati aliwatembelea. Alisema kusudi lake lilikuwa "kuleta utiifu wa imani" (16:26).

Katika barua hii Paulo alieleza kikamilifu Injili ya Yesu Kristo. Alielezea kuwa Wayahudi na Wayunani wamefanya dhambi, na Mungu atawasamehe na kuwaita wenye haki tu ikiwa wanaamini Yesu (sura ya 1-11). Kisha akawapa maelekezo ya manufaa kuhusu jinsi waumini wanapaswa kuishi (sura 12-16),

Je, kichwa cha kitabu hiki kinapaswa kutafsiriwaje?

Watafsiri wanaweza kuchagua kuita kitabu hiki kwa kichwa chake asilia, "Warumi." Au wanaweza kuchagua kichwa kilicho wazi zaidi, kama "Barua ya Paulo kwa Kanisa la Roma," au "Barua kwa Wakristo huko Roma." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-names)

Sehemu ya 2: Dhana muhimu za Kidini na za Kitamaduni

Je, ni majina yapi yanayotumiwa kumtaja Yesu?

Katika Warumi, Paulo alielezea Yesu Kristo kwa majina mengi na maelezo: Yesu Kristo (1:1), Ukoo wa Daudi (1:3), Mwana wa Mungu (1:4), Bwana Yesu Kristo (1:7) , Kristo Yesu (3:24), Dhabihu ya upatanisho (3:25), Yesu (3:26), Yesu Bwana wetu (4:24), Bwana wa Majeshi (9:29), Jiwe la Kujikwaa na Mwamba wa Kosa (9:33), Mwisho wa Sheria (10:4), Mkombozi (11:26), Bwana wa Wafu na Wanaoishi (14:9), na Shina la Yese (15:12).

Je, maneno ya kidini katika Warumi yanapaswa kutafsiriwaje?

Paulo anatumia maneno mengi ya kitheolojia ambayo haitumiwi katika injili nne. Kama Wakristo wa mapema walijifunza zaidi juu ya maana ya Yesu Kristo na ujumbe wake, walihitaji maneno na maelezo kwa mawazo mapya. Baadhi ya mifano ya maneno haya ni "kuhesabiwa haki" (5:1), "kazi za sheria" (3:20), "dhabihu ya upatanisho" (5:10), "ukombozi" (3:25), "utakaso" (6) : 19), na "mwili wa asili" (6: 6).

Kamusi ya "maneno muhimu" inaweza kuwasaidia watafsiri kuelewa baadhi ya maneno haya. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-abstractnouns)

Maneno kama yale yaliyopewa hapo juu ni magumu kuelezea. Mara nyingi ni vigumu au haiwezekani kwa watafsiri kupata maneno sawa na hayo katika lugha zao wenyewe. Inaweza kusaidia kujua kwamba maneno yaliyo sawa na maneno haya hayahitajiki. Badala yake, watafsiri wanaweza kuunda misemo mifupi ili kuweza kuwasiliana mawazo haya. Kwa mfano, neno "injili" linaweza kutafsiriwa kama "habari njema juu ya Yesu Kristo."

Watafsiri pia wanapaswa kukumbuka kwamba baadhi ya maneno haya yana maana zaidi ya moja. Maana yatategemea jinsi mwandishi anatumia neno katika kifungu fulani. Kwa mfano, "haki" wakati mwingine ina maana kwamba mtu hutii sheria ya Mungu. Wakati mwingine, "haki" inamaanisha kwamba Yesu Kristo ametii kikamilifu sheria ya Mungu kwa niaba yetu.

Paulo alimaanisha nini aliposema "waliosalia" wa Israeli (11:5)?

Wazo la "mabaki" ni muhimu katika Agano la Kale na kwa Paulo. Waisraeli wengi walikuwa wameuawa au kutawanyika kati ya watu wengine wakati Waashuri na kisha Wababiloni walinyakua ardhi yao. Wayahudi wachache tu walibakia. Walijulikana kama "waliosalia."

Katika 11:1-9, Paulo anazungumzia waliosalia wengine. Hawa ni Wayahudi ambao Mungu aliwaokoa kwa sababu waliamini Yesu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#remnant)

Sehemu ya 3: Masuala muhimu ya Tafsiri

Paulo alimaanisha nini aliposema kwa kuwa "katika Kristo"?

Maneno "katika Kristo" na maneno kama hayo yapo katika 3:24; 6:11, 23; 8:1,2,39; 9:1; 12:5,17; 15:17; na 16:3,7,9,10. Paulo alitumia maneno haya kama mfano ili kuonyesha kwamba waumini Wakristo ni wa Yesu Kristo. Kuwa wa Kristo inamaanisha mwamini anaokolewa na hufanywa rafiki na Mungu. Muumini pia ameahidiwa kuishi na Mungu milele. Hata hivyo, wazo hili linaweza kuwa vigumu kuwakilisha katika lugha nyingi.

Misemo hii pia ina maana maalum ambazo hutegemea jinsi Paulo aliyotumia katika kifungu fulani. Kwa mfano, katika 3:24 ("ukombozi ulioko ndani ya Kristo Yesu"), Paulo alimaanisha kuokolewa kwetu "kwa sababu" ya Yesu Kristo. Katika 8:9 ("ninyi hamko katika mwili bali katika Roho"), Paulo alizungumza juu ya waumini wanaomtii Roho Mtakatifu. Katika 9:1 ("Ninasema ukweli katika Kristo"), Paulo alimaanisha kuwa anasema ukweli ambao "unakubaliana na" Yesu Kristo.

Hata hivyo, wazo la msingi la sisi kuwa kwa umoja na Yesu Kristo (na kwa Roho Mtakatifu) linaoneka katika vifungu hivi pia. Kwa hiyo, mtafsiri ana uhuru wa kuchagua katika vifungu vingi vinavyotumia "ndani." Mara nyingi huamua kutumia maana ya karibu sana ya "ndani," kama, "kwa njia ya," "kwa namna ya," au "kuhusiana na." Lakini, ikiwa inawezekana, mtafsiri anapaswa kuchagua neno au maneno ambayo yanaelezea maana ya karibu sana na maana ya "umoja na." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#inchrist)

Je, namuna gani mawazo ya "takatifu," "watakatifu" au "walio watakatifu," na "kutakasa" yanawakilishwa katika Warumi katika ULB?

Maandiko hutumia maneno kama hayo ili kuelezea moja kati ya mawazo mbalimbali. Kwa sababu hii, mara nyingi ni vigumu kwa watafsiri kuyawakilisha vizuri katika matoleo yao. Katika kutafsiri kwa Kiingereza, ULB inatumia kanuni zifuatazo:

UDB mara nyingi husaidia ikiwa watafsiri wanawaza jinsi ya kuwakilisha mawazo haya katika tafsiri za lugha zao.

Je, ni yapi masuala makuu katika maandishi ya Kitabu cha Warumi?

Yafuatayo ni masuala ya muhimu zaidi katika Kitabu cha Warumi:

Watafsiri wanashauriwa kutotafsiri kifungu hiki. Hata hivyo, ikiwa katika eneo la watafsiri, kuna matoleo ya zamani ya Biblia ambayo yanajumuisha kifungu hiki, watafsiri wanaweza kuijumuisha. Ikiwa zinatafsiriwa, zinapaswa kuwekwa ndani ya mabano ya mraba ([]) ili kuonyesha kwamba labda asili yao sio Kitabu cha Warumi. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/jit.html#translate-textvariants)

(See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/jit.html#translate-textvariants)

Romans 1

Warumi 01 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Mstari wa kwanza ni aina ya utangulizi. Watu katika eneo la kale la Mediterania mara nyingi walianza barua zao kwa njia hii. Wakati mwingine hii inaitwa "salamu."

Dhana maalum katika sura hii

Injili

Sura hii inaashiria yaliyomo katika Kitabu cha Warumi kuwa "Injili" (Warumi 1:2). Kitabo cha Warumi sio injili kama Mathayo, Marko, Luka na Yohana. lakini, sura za 1-8 zinawasilisha injili ya kibiblia: Wote wametenda dhambi. Yesu alikufa kwa ajili ya dhambi zetu. Alifufuliwa tena ili tuweze kuwa na maisha mapya ndani yake.

Matunda

Sura hii inatumia mfano ya matunda. Mfano wa matunda mara nyingi inahusu imani ya mtu inayozalisha matendo mema katika maisha yake. Katika sura hii, inahusu matokeo ya kazi ya Paulo kati ya Wakristo wa Kirumi. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#fruit and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous)

Ushtakiwa wa Ujumla na Ghadhabu ya Mungu

Sura hii inaeleza kwamba hakuna mtu aliye na udhuru. Sisi sote tunajua kuhusu Mungu wa kweli, Yahweh, kutoka kwa viumbe vyake vilivyopo karibu na sisi. Kwa sababu ya dhambi zetu na asili yetu ya dhambi, kila mtu hakika anastahili ghadhabu ya Mungu. Ghadhabu hii ilidhihirishwa na Yesu akifa msalabani kwa wale wanaomwamini. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#believe and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

Mifano muhimu ya matamshi katika sura hii

"Mungu aliwapa"

Wasomi wengi wanaona maneno "Mungu aliwaacha" na "Mungu aliwaacha kufuata" kama maneno muhimu ya kitheolojia. Kwa sababu hii, ni muhimu kutafsiri maneno haya yakionyesha Mungu kutokuwa mtendaji mkuu. Hapa Mungu anaruhusu tu watu kufuata tamaa zao wenyewe, yeye hawalazimishi. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-activepassive)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Misemo na dhana ngumu

Sura hii ina mawazo mengi magumu ndani yake. Jinsi Paulo anavyoandika hufanya maneno mengi katika sura hii kuwa vigumu kutafsiri. Labda mtafsiri anahitaji kutumia UDB kuelewa maana ya maneno. Na inaweza kuwa muhimu zaidi kutafsiri maneno haya kwa uhuru. Baadhi ya maneno magumu yanajumuisha: "utiifu wa imani," "ninayemtumikia katika roho yangu," "kutoka kwa imani hadi imani" na "kubadilishana utukufu wa Mungu asiyeharibika kwa mfano wa mtu anayeharibika."

| >>

Romans 1:1

Paulo

Lugha yako inaweza kuwa na namna ya kumtambulisha mwandishi wa barua. "Mimi Paulo naandika barua hii." Unaweza pia kusema ni kwa nani barua iliandikwa.

kuitwa kuwa mtume, na kutengwa kwa ajili ya injili ya Mungu

"Mungu alinita mimi kuwa mtume na alinichagua kuwaambia watukuhusu injili"

Kuitwa

Hapa inamaana kuwa Mungu aliteua au kuchagua watu kuwa watoto wake, kuwa watumishi wake na watangazaji wa ujumbe wake wa wokovu kupitia kwa Yesu.

Hii ni injili ambayo aliiahidi kabla kwa mitume wake kwenye maandiko matakatifu

Mungu aliwaahidi watu wakekwamba atawaandalia ufalme. Aliwaambia mitume waandike ahadi hizi kwenye maandiko.

Ni kuhusu mwana wake

Hii inamaanisha "Injili ya Mungu," habari njema ambayo Mungu aliwaahidi kuwapa mwanawe ulimwenguni.

Mwana

Hiki ni cheo cha muhimu sana kwa Yesu, Mwana wa Mungu.

Aliyezaliwa toka kwa uzao wa Daudi kutokana na mwili

Hapa neno "mwili" linamaanisha mwili unaoonekana. "Ambaye ni uzao wa Daudi kutokana na asili ya mwili" au "aliyezaliwa kwenye familia ya Daudi."

Romans 1:4

Maelezo yanayounganisha:

Paulo anazungumza kuhusu majukumu yake katika kuhubiri.

Alithibitishwa kuwa mwana wa Mungu.

Neno "yeye" linamaanisha Yesu. "Mungu alimthibitisha yeye kuwa mwana wa Mungu"

Mwana wa Mungu

Ufufuo wa Yesu unathibitisha kuwa alikuwa na ndiye "mwana wa Mungu." Hiki ni cheo cha muhimu sana cha Yesu.

Roho ya utakatifu

Hii inmaanisha roho mtakatifu.

kwa ufufuo wa wafu

"kwa kuleta tena kwenye uhai baada ya kufa"

Tumepokea neema na utume

"Alinichagua mimikuwa mtume" au "Mungu alinipa zawadi ya neema ya kuwa mtume." "Mungu kwa neema yake alinipa zawadi"

Sisi

Hapa neno "sisi" linamaanisha Paulo na mitume 12 waliomfuata Yesu lakini ukiwatoa waamini katika kanisa la Roma.

kwa kutii imani kati ya mataifa yote, kwa ajili ya jina lake.

Paulo anatumia neno "jina" akiwa anamzungumzia Yesu. "kwa ajili yakuwafundisha mataifa yote kutii kwa sababu ya imani yao kwake"

Romans 1:7

Barua hii ni kwa ajili ya wpote waliopo Roma, wapendwa wa Mungu, walioitwa kuwa watu watakatifu

"Naandika barua hii kwenu nyote mliopo Roma ambao mnapendwa na Mungu na mmechaguliwa kuwa watu wake"

Neema iwe kwenu, na amani

"Neema na amani iwe kwenu"

Romans 1:8

Ulimwengu wote

Hii inamaanisha ulimwengu walioufahamu, ambao ni ngome wa Roma.

Kwa kuwa Mungu ni shahidi yangu

Paulo anasisitiza kwamba ameomba kwa bidii kwa ajili yao na kwamba Mungu alimuona akiwa anaomba.

Kwa roho yangu

Hapa inamaanisha roho ya mtu ni sehemu yake ambayo inamtambua Mungu na kumwamini.

Injili ya mwanawe

Habari njema (injili) ya Biblia ni kwamba mwana wa Mungu alijitoa mwenyewe kama mkombozi wa dunia.

Mwana

Hiki ni cheo cha muhimu sana kwa Yesu, Mwana wa Mungu.

Nakutaja wewe

"Niliongea na Mungu kuhusu wewe"

Kila mara kwenye maombi yangu nimekuwa nikiomba kuwa.. Hatimaye nifanikiwe... kuja kwako

Kila mara naomba, na kumwambia Mungu kwamba... Nifanikiwe... kuja kukutembelea wewe"

Kwa njia yoyote

"Kwa njia yoyote ambayo Mungu ataruhusu"

Hatimaye

"mwisho"

Kwa mapenzi ya Mungu

"kwa sababu Mungu ametamani hivyo"

Romans 1:11

Sentensi unganishi:

Paulo anaendelea kuweka wazi maelezo yake kwa watu wa Rumi kwa kuelezea shauku yake ya kuwaona mmoja mmoja.

Kwa kuwa natamani kuwaona

"kwa kuwa nataka kuwaona"

Kwa kuwa

"kwa sababu"

baadhi ya zawadi za roho, ili kuwatia nguvu

"baadhi ya zawadi toka kwa Roho Mtakatifu, ambayo itawasaidia na kuwatia nguvu"

Ambayo ni, mfarijiane kati yenu, kupitia imani ya kila mtu, yenu na yangu

"Namaanisha kwamba nataka tutiane moyo kwa kutumia uzoefu wa imani yetu kwa Yesu"

Romans 1:13

Sitaki msifahamu

Paulo anasisitiza kwamba alitaka wawe na taarifa hii. "Nilitaka ninyi mfahamu haya"

Ndugu

Hapa anamaanisha Wakristo wenzake, ukijumuisha wote wanaume na wanawake.

Lakini nilikuwa nimezuiwa

"kuna kitu kilikuwa kinanizuia"

Muwe na tunda

"Tunda" linawakilisha watu wa Roma amabao Paulo alitaka kuwaongoza waamini injili.

Kama ilivyo kati ya Mataifa

"Kama ambavyo watu walikuja kuamini injili kwemye taifa lingine la Mataifa"

Nina deni kwa wote

"Lazima nipeleke injili kwa"

Romans 1:16

Siionei haya injili

"Nina ujasiri ninapoongea kuhusu injili, japokuwa watu wengi wanakataa"

Kwa kuwa siionei haya

Paulo anaelezea kwa nini anataka kuhubiri injili Roma.

Kwa kuwa ndani yake

Hii inaelezea injili. Paulo anaelezea kwa nini anahubiri injili kwa ujasiri.

Ni nguvu ya Mungu ya wokovu kwa kila mtu anayeamini

"Ni kupitia injili nguvu ya Mungu inawaokoa wanaomwamini Kristo"

Kwa Wayahudi kwanza na kwa Wagiriki

"kwa watu wa Kiyahudi na watu wa Kigiriki"

Kwanza

Hii inaweza kuwa na maana kuwa 1) "ya kwanza kwa sababu ya mda" au 2) "ya muhumu sana"

Haki ya Mungu inadhihirishwa toka imani mpaka imani

"Mungu amedhihirisha kuwa ni kwa imani toka mwanzo mpaka mwisho watu wanakuwa na haki" "Mungu amedhihirisha haki yake kwa wale walio na imani, na matokeo yake wanaimani zaidi" au "kwa sababu Mungu ni mwaminifu, amedhihirisha haki yake, na matokeo yake watu wamekuwa na imani zaidi"

Mwenye haki ataishi kwa imani

"Ni watu wanaomwamini Mungu ndio anaowaona wenye haki, na wataishi milele"

Romans 1:18

Sentensi unganishi:

Paulo anadhihirisha hasira kuu ya Mungu dhidi ya wanaotenda dhambi.

Kwa kuwa ghadhabu yake

Paulo anaelezea kwa nini watu wanatakiwa kuisikia injili.

Ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa

"Mungu amedhihirisha hasira yake"

Dhidi

"juu ya"

uasi wote na udhalimu wa watu

"uasi wote na mambo ya udhalimu ambayo watu wanayatenda"

kuuficha ukweli

"walificha taarifa za kweli kuhusu Mungu"

ambayo inajulikana kuhusu Mungu inaonekana kwao

"wanaweza kujua kuhusu Mungu kwa sababu ya wanayoyaona"

Kwa kuwa Mungu

Paulo anawaonyesha kwa nini watu wanajua mambo kuhusu Mungu.

Mungu amewaangazia

"Mungu ameyaonyesha hayo kwao"

Romans 1:20

Kwa kuwa

Paulo anaelezea namna ambavyo Mungu alijidhihirisha mwenyewe kwa wanabamu

Mambo yake yasiyoonekana yameonekana wazi

"mambo yasiyoonekana" ni mambo yasiyoonekana kwa macho. Yamekuwa "yameonekana wazi" kwa sababu watu wameelewa kuwa wako pale japokuwa hawawezi kuona kwa macho yao.

Ulimwengu

Hii inamaanisha mbingu na dunia, pamoja na vyote vilivyomo.

Asili ya Mungu

"Ubora na tabia za Mungu" au "mambo ya Mungu yanayomfanya awe Mungu"

Wanaelewe kupitia vitu vilivyoumbwa

"watu wanaweza kuelewa kuhusu Mungu kwa kuangalia vitu alivyovifanya"

Watu hawa hawatakuwa na udhuru

"Watu hawa hawatasema kuwa hawakujua"

Wakawa wajinga kwenye mawazo yao

"wakaanza kuwaza mambo ya kijinga"

Mioyo yao isiyo na hisia ilikuwa na giza

Maelezo haya yanaonyesha moyo uliokuwa na giza ikimaanisha wamekosa uelewa. "mioyo yao haiwezi tena kuelewa"

Romans 1:22

Wanadai kuwa na hekima, lakini wakawa wajinga.

"Walipokuwa wanadai kuwa wana hekima, wakawa wajinga"

Wao...wao

Watu

Wakabadilisha utukufu usioharibika

"wakauza ukweli kuwa Mungu ni mtukufu na hatakufa" au "wakaacha kuamini kuwa Mungu ni mtukufu na hatakufa"

kwa kufananisha na sura ya

"na badala yake walichagua kuabudu sanamu waliotengenezwa kufanana na"

mtu anayeharibika

"mtu ambaye atakufa"

Romans 1:24

Kwa hiyo

"kwa sababu hii"

Mungu aliwapa ili

"Mungu aliwaruhusu wajiingize" au Mungu aliruhusu"

Wao...yao...wenyewe...wale

"binadamu"

Tamaa za mioyo yao kwa uchafu

"Vitu vya maadili machafu walivyotamani kuwa navyo"

kwa miili yao kufedheheshwa kati yao wenyewe

Walifanya matendo ya mwili yasiyofaa na udhalilishaji.

badala ya

Inaweza kuwa na maana 1) "badala ya" au 2) "pamoja na"

Romans 1:26

Hii

"uzinzi na dhambi ya uasherati"

Mungu aliwapa ili

"Mungu aliruhusu wajiingize"

Tamaa ya kufedhehesha

"tamaa za aibu za kimwili"

Kwa kuwa wanawake wao

"kwa sababu wanawake wao"

Wanawake wao

wanawake wa "mwanadamu"

Wakageuza matumizi ya asili kinyume na asili

"Wakaanza kujamiiana kwa njia ambayo Mungu hakuitengeneza"

Wakaungua kwa tamaa zao

"wakapata tamaa kali za mwili"

Isivyofaa

"kudhalilisha" au "chafu" au "dhambi"

Waliopokea adhabu kwa sababu ya upotoshaji wao

"Waliopokea adhabu inayostahili toka kwa Mungu kwa sababu ya upotoshaji wao"

kupotosha

Tabia ambayo ni mbaya na isiyofaa.

Romans 1:28

Kwa sababu hawakuthibitisha kuwa na Mungu katika ufahamu wao

"Hawakufikiri kuwa kulikuwa na umuhimu wa kumjua Mungu"

Wao...yao...wale

Maneno haya yanamaanisha "binadamu"

Aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa

Mungu aliruhusu akili zao zijazwe na uasherati na uwatawale"

sio sahihi

"kudhalilisha" au "isiyo na heshima" au "dhambi"

Romans 1:29

Walijazwa na

"Ndani yao walikuwa wanatamani" au "walikuwa na matamanio makubwa ya kufanya matendo ya"

Romans 1:32

Wanaelewa taratibu za Mungu

Wanajua kuwa Mungu anataka waishi kwenye njia zake za haki.

kufanya mambo hayo

"kufanya matendo maovu"

Kustahili kifo

"wanastahili kufa"

Romans 2

Warumi 02 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Sura hii inabadilisha wasikilizaji wake kutoka kwa Wakristo wa Kirumi na kuwa wale ambao "wanahukumu" watu wengine na hawaamini Yesu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#judge and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#believe)

"Kwa hiyo huwezi kamwe kujitetea"

Kifungu hiki kinatazama nyuma katika Sura ya 1. Kwa njia fulani, kwa kweli huhitimisha kile Sura ya 1 inafundisha. Kifungu hiki kinafafanua kwa nini kila mtu duniani lazima aabudu Mungu wa kweli.

Dhana maalum katika sura hii

"Wenye kuitii sheria"

Wale ambao wanajaribu kutii sheria hawatahesabiwa haki kwa kujaribu kuiitii. Wale ambao wanahesabiwa haki kwa kumwamini Yesu wanaonyesha kwamba imani yao ni ya kweli kwa kutii amri za Mungu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#justice and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lawofmoses)

Mifano muhimu ya matamshi katika sura hii

Maswali ya uhuishaji

Paulo anatumia maswali kadhaa ya uhuishaji katika sura hii. Inaonekana nia ya maswali haya ya uhuishaji ni kufanya msomaji kuona dhambi zake ili amtegemee Yesu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-rquestion, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#guilt and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith)

Hali ya Kufikiri

Katika muktadha, "atatoa uzima wa milele" katika mstari wa 7 ni tamko la kufikiri. Ikiwa mtu anaweza kuishi maisha kamilifu, angepata uzima wa milele kama tuzo. Lakini Yesu peke yake alikuwa na uwezo wa kuishi maisha kamilifu.

Paulo anatoa hali nyingine ya kufikiri katika mstari wa 17-29. Hapa anaelezea kuwa hata wale wanaojitahidi kufuata sheria ya Musa wana hatia ya kukiuka sheria. Kwa Kiingereza, hii inahusu wale wanaofuata "maandiko" ya sheria lakini hawawezi kufuata "roho" au kanuni za jumla za sheria. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-hypo)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Nyinyi mnaohukumu"

Wakati mwingine, hii inaweza kutafsiriwa kwa njia rahisi. Lakini inatafsiriwa kwa njia hii isiyo ya maana kwa sababu wakati Paulo akimaanisha "watu wanaohukumu" anasema pia kila mtu anahukumu. Inawezekana kutafsiri hii kama "wale wanaohukumu (na kila mtu anahukumu)."

<< | >>

Romans 2:1

Sentensi unganishi:

Paulo amesema kuwa wato wote ni wenye dhambi na anaendelea kuwakumbusha kuwa watu wote ni waovu.

Kwa hiyo umekosa sababu ya kujitetea

Neno "kwa hiyo" linaonyesha sehemu mpya ya barua. Inaonyesha suluhisho la sentensi ikionyesha yaliyosemwa "tangu Mungualipowaadhibu watu wanaoendelea kutenda dhambi, na hataonea huruma kwa sababu ya dhambi zao"

Wewe ni

Paulo haongei na mtu. Anajifanya kama Myahudi anayelumbana naye. Paulo anafanya haya kuwafundisha wasikilizaji wake kuwa Mungu atamhukumu kila mtu anayeendelea kutenda dhambi, awe Myahudi au wa Mataifa.

Wewe

Hapa neno "wewe" ni umoja.

Wewe mtu, wewe unayehukumu

Hapa neno "mtu" ilitumika kumdhihaki mtu aliyefikiri anaweza kufanya kama Mungu na kuwahukumu wengine. "Wewe ni binadamu tuu, lakini unawahukumu wengine na kusema kuwa wanastahili hukumu ya Mungu"

kwa unavyohukumu kwa wengine unahukumu kwako mwenyewe.

"Lakini unajihukumu mwenyewe kwa sababu unafanya mambo maovu kama wanavyofanya wengine"

Lakini twajua

Hii inajumuisha Wakristo walioamini na Wayahudi ambao sio Wakristo.

Hukumu ya Mungu ni kutokana na kweli ikiwaangukia wao

"Mungu atawahukumu watu kwa kweli na haki"

Wale wanaofanya mambo hayo

"watu wanaofanya mambo maovu"

Romans 2:3

Lakini

"kwa hiyo"

Fikiria hili.

"fikiria kuhusu hili ninalokwenda kukwambia"

Mtu

Tumia neno la jumla kwa binadamu.

Wewe unayewahukumu wanaofanya mambo hayo japokuwa na wewe unafanya vivyo hivyo.

"Wewe unayesema mtu anastahili adhabu ya Mungu wakati unafanya mambo maovu"

Je utaepuka hukumu ya Mungu?

"hautaepuka hukumu ya Mungu!"

Au unadharau utajiri wa wema wake, na hukumu yake iliyochelewa, na uvumilivu... tubu?

"Unajifanya kama hujali kwamba Mungu nimwema na ni mvumilivu akisubiria muda mrefu kabla ya kuwahukumu watu, kwa hiyo wema wake utasababisha watu watubu."

Unadharau utajiri wake... uvumilivu

"fikiria utajiri... uvumilivu sio muhimu" au "fikiria... sio vizuri"

HaUjui kuwa wema wake una maana ya kukusababisha utubu?

"Unatakiwa ufahamu kuwa Mungu anakuonyesha kuwa ni mwema hivyo utubu."

Romans 2:5

Sentensi unganishi:

Paulo anaendelea kuwakumbusha watu kwamba watu wote ni waovu.

Lakini ni kwa kadri ya ugumu wako na moyo wako usiotubu

Paulo anamfananisha mtu aliyekataa kusikia na kumtii Mungu na kitu kigumu, kama jiwe. Moyo unamaanisha mtu mzima. "Ni kwa sababu umekataa kusikiliza na kutubu"

Ugumu na moyo usiotubu

Mstari "moyo usiotubu" inaelezea neno "ugumu"

Unajiwekea mwenyewe akiba ya ghadhabu

Neno "kujiwekea" inamaanisha mtu aliyekusanya mali zake na kuziweka sehemu salama. Paulo anasema badala ya mali mtu anakusanya adhabu ya Mungu. Kadri unavyoendelea bila kutubu, ndivyo adhabu inavyozidi kuwa kubwa. "unaifanya adhabu yako inakuwa mbaya zaidi"

siku ya ghadhabu... siku ambayo Mungu atadhihirisha hukumu yake ya haki

Hii inamaanisha siku hiyo hiyo. "Ambayo Mungu atawaonyesha watu kuwa ana hasira na anahukumu watu wote kwa haki."

Kulipa

"Kutoa tuzo ya haki au adhabu"

kwa kila mtu kipimo sawa kwa matendo yake

"kutokana na kila mtu alivyofanya"

Wametafuta

Hii inamaanisha kwamba walienenda kwa njia ambazo ziliwapa matokeo hasi toka kwa Mungu siku ya hukumu.

Sifa, heshima na kutokuharibika.

Walitaka Mungu awasifu na kuwaheshimu, na walitaka wasife kabisa.

Kutoharibika

Hii inamaanisha, kimwili, sio ya maadili, kuoza.

Romans 2:8

Sentensi unganishi:

Japokuwa sehemu hii inazungumzia watu waovu wasio na dini, Paulo anajumuisha kuwa wote wasio Wayahudi na Wayahudi ni waovu mbele za Mungu.

Ubinafsi

Kujitafutia, "choyo" au "mtu anayejali kujipa furaha yeye mwenyewe"

Kutokutii ukweli lakini kutii wasio na haki

Mistari hii miwili ina maana sawa. Ya pili inaelezea ya kwanza.

Ghadhabu na hasira kali itakuja

yanamaanisha kitu kimoja na yanasisitiza hasira ya Mungu. "Mungu ataonyesha hasira yake kuu"

Dhiki na shida juu ya

Maneno "dhiki" na "shida" yana maana sawa na hapa yansisitiza namna mbavyo adhabu ya Mungu itakavyokuwa mbaya. "Adhabu mbaya ya Mungu itatokea"

Kwa kila nafsi ya mwanadamu

Hapa Paulo ametumia neno "nafsi" kuonyesha kuwa anamaanisha mtu kwa ujumla. "kwa kila mtu"

Amefanya uovu

"ameendelea kufanya mambo maovu"

Kwa Wayahudi kwanza , na pia kwa Wayunani

"Mungu atawahukumu Wayahudi kwanza, na baada ya hapo atawahukumu ambao sio Wayahudi"

Kwanza

Inaweza kuwa na maana 1) "ya kwanza kwa utaratimu na wakati" au 2) "hakika" au "ya muhimu sana"

Romans 2:10

Lakini sifa, heshima na amani vitakuja.

"Lakini Mungu atatoa sifa, heshima na amani"

Tenda mema

"endeleeni kufanya yaliyo mema"

Kwa Wayahudi kwanza , na pia kwa Wagiriki

"Mungu atawapa tuzo Wayahudi kwanza, na baada ya hapo ambao sio Wayahudi"

Kwa maana hakuna upendeleo kwa Mungu

"Kwa kuwa Mungu hapendelei baadhi ya watu juu ya wengine" au "kwa kuwa Mungu anausawa kwa watu wote"

Kwa wingi wao kama walivyotenda dhambi

"Kwa wale walotenda dhambi"

Bila sheria pia wataangamia bila sheria

Paulo anarudia "bila sheria" ili kusisitiza kuwa haijalishi kama hawajui sheria ya Musa. Kama wakitenda dhambi Mungu atawahukumu. "Bila kujua sheria za Musa bado watakufa kiroho"

na wingi wao kama walivyotenda dhambi

"Na wote waliotenda dhambi"

Kwa kutii sheria watahukumiwa kwa sheria

"Na kujua sheria za Musa, Mungu atawahukumu kutokana na sheria ya Musa.

Romans 2:13

Sentensi unganishi:

Paulo anaendelea kuwafanya wasomaji wajue kwamba kutii sheria za Mungu inatakiwa hata kwa wale ambao hawana sheria za Mungu.

Kwa

Kama lugha yako ina njia nyingine aya kuelezea kuwa mstari wa 14 na 15 unaingilia mawazo makuu ya Paulo na kumpa msomaji taarifa za ziada. Unaweza ukaiweka 2:14-15 kabla ya 2:13 au baada ya 2:16. "kwa sababu"

Sio wasikilizaji wa sheria

"Sio tuu kwa wale wasikilizaji wa sheria ya Musa"

Walio na haki mbele za Mungu

"wale wanaompendeza Mungu"

lakini ni kwa watendaji wa sheria

"lakini ni kwa wale wanaoitii sheria ya Musa"

Kina nani watakuwa waadilifu.

"ambao Mungu atawapokea"

Walio na sheria kwao wenyewe

"Walio na sheria za Mungu ndani mwao"

Romans 2:15

Kwa hili walionyesha

"Kwa kutii sheria walionyesha"

Matendo yaliyotakiwa na sheria yaliyoandikwa kwenye mioyo yao

"Mungu ameandika kwenye mioyo yao mambo ambayo sheria inawataka wafanye" au "Walifahamu ni nini sheria iliwataka wao wafanye"

Yaliyotakiwa na sheria

"Sheria inataka" au "Ambayo Mungu ameamuru kupitia sheria"

kuwashuhudia wao, na mawazo yao wenyewe ama kuwashitaki au kuwalinda kwa ajili yao wenyewe

"waambie kama hawatii au wanatii amri za Mungu"

Siku ambayo Mungu atahukumu

Hii inaelezea mwisho wa mawazo ya Paulo "hii itatokea siku ambayo Mungu atahukumu"

Romans 2:17

Ikiwa wewe unajiita Myahudi

Hapa neno "kama" haimaanishi Paulo ana mashaka au hana uhakika. Anasisitiza kuwa sentensi hii ni ya kweli. "Sasa mnajiona wenyewe kama watu watu wa Kiyahudi."

Kutegemea torati, kujisifu kwa furaha katika Mungu

"na ninyi mnategemea sheria ya Musa na kujisifu kwa furaha kwa sababu ya Mungu"

Kujua mapenzi yake

"Na nyie kujua mapenzi ya Mungu"

kama mlivyoelekezwa na sheria

"kwa kuwa mmeelewa ni nini sheria ya Musa inafundisha"

Ikiwa una ujasiri... na ukweli

Kama lugha yako ina namna ya kutafsiri maelezo ya Paulo kwenye sura ya 2:19-20. unaweza kuweka 2:19-20 kabla ya 2:17.

Kwamba ninyi wenyewe ni viongozi wa vipofu, mwanga kwa walio gizani.

Sentensi hizi zina maana inayofanana. Paulo anafananisha Myahudi anayemfundisha mtu kuhusu sheria kumsaidia mtu ambaye haoni. "kwamba ninyi wenyewe ni kama viongozi kwa mtu aliye kipofu, na ni mwanga kwa mtu aliyepotea gizani"

Mkufunzi wa wajinga

"Unawarekebisha wale wanaofanya makosa"

Mwalimu wa watoto

Hapa Paulo anawafananisha wale wasiojua chochote kuhusu sheria kama watoto. "na uwafundishe wale wasiojua sheria"

na mlichonacho kwenye sheria maarifa na kweli

"kwa sababu mna hakika kuwa mnaelewa ukweli ulioandikwa kwenye sheria"

Romans 2:21

Wewe, pia, unayefundisha watu, haujifunzi mwenyewe?

Paulo alitumia swali kuwakemea wasikilizaji wake. "Lakini haujifunzi wenyewe wakati unawafundisha wengine!"

Wewe unayehubiri mtu asiibe, je unaiba?

Paulo alitumia swali kuwakemea wasikilizaji wake. "Unawaambia watu wasiibe, lakini wewe unaiba!"

Wewe unayehubiri mtu asizini, je unazini?

Paulo alitumia swali kuwakemea wasikilizaji wake. "Unawaambia watu wasizi, lakini wewe unazini!"

Nyie mnaochukia sanamu, je mnaiba mahekalu?

Paulo anatumia swali kuwakemea wasikilizaji wake. Mnasema mnachukia sanamu, lakini mnaiba mahekalu!"

Mnaiba mahekalu

Inaweza kuwa na maana 1) "kuiba vitu toka kwenye mahekalu ya wapagani kuviuza na kupata faida" au 2) "msipeleke kwenye hekalu la Yerusalemu pesa zote ambazo ni za Mungu" au 3) "kufanya mzaha kuhusu miungu."

Romans 2:23

Ninyi mnaojisifu kwa furaha kwenye sheria, je hamumtii Mungu kupitia uvunjaji wenu wa sheria?

Paulo anatumia swali kuwakemea wasikilizaji wake. "Ni uovu mnavyojifanya mnajivunia kwa sheria, wakati huo huo hamuitii na kuleta aibu kwa Mungu."

Jina la Mungu haliheshimiwi kati ya Mataifa

"Matendo yenu maovu yanaleta aibu kwa Mungu kwenye fikra za Mataifa"

Jina la Mungu

Neno "Jina" linamaanisha umilele wa Mungu, sio tuu jina lake.

Romans 2:25

Maelezo yanayounganisha:

Paulo anaendelea kuonyesha kwamba Mungu, kwa sheria zake, anawaadhibu hata Wayahudi ambao wana sheria za Mungu.

Kwa kuwa tohana imekupa faida wewe

"Nasema haya yote kwa sababu kutahiriwa kumekupa faida"

Kama ukiwa mkiukaji wa sheria

"Kama usipotii amri zilizopo katika sheria"

Kutahiriwa kwako kutakuwa kutokutahiriwa

Hii inamfananisha Myahudi asiyetii sheria na mtu ambaye ametahiriwa lakini anaonekana kama hajatahiriwa : anaweza kuwa Myahudi lakini akaishi kama mtu wa Mataifa. "Ni kama vile haujatahiriwa"

Mtu asiyetahiriwa

"Mtu ambaye hajatahiriwa"

Kuyashika maagizo ya sheria

"kutii kilichoamriwa kwenye sheria"

kutokutahiriwa kwake hakuwezi kuchukuliwa kama kutahiriwa? Na ambaye hajatahiriwa kwa asili hawezi kukuhukumu... sheria?

Paulo aliuliza maswali mawili kusisitiza kuwa kutahiriwa sio jambo la kumfanya mtu kuwa na haki mbele za Mungu. "Mungu atamchukulia kama mtu aliyetahiriwa.... na mtu ambaye hajatahiriwa ... atakuhukumu... sheria."

Romans 2:28

Kwa nje

Hii inamaanisha mambo ya nje ya Kiyahudi ambayo watu wanayaona.

Siyo ya nje tuu katika mwili

Hii inamaanisha mabadiliko ya nje katika mwili wa binadamu.

Ni Myahudi kwa ndani, na tohara ni ile ya moyoni

Mistari hii miwili ina maana inayofanana. Mstari unaosema, "Ni Myahudi kwa ndani," inaelezea kuwa, "tohara ni ile ya moyoni."

Ndani

Hii inaonyesha thamani na motisha ya mtu ambaye Mungu amembadilisha.

Kwa Roho, sio kwenye barua

"Barua" ni sehemu ndogo ya maandishi katika lugha. Hapa inamaanisha maandiko. "kupitia kazi ya roho mtakatifu, sio kwa sababu unajua maandiko."

Kwa Roho

Hii inaweza kuwa na maana ya ndani, sehemu yakiroho ya mtu, tofauti na nje "barua" ya sheria. Pia inamaana ya Roho Mtakatifu.

Romans 3

Warumi 03 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri huweka kila mstari wa mashairi kwenye upande wa kulia zaidi ya maandiko yote ili iwe rahisi kusoma. ULB inafanya hili kwa mistari ya 4 na 10-18 ya sura hii, ambayo ni maneno kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

Sura ya 3 hujibu swali hili, "Ni faida gani kuwa Myahudi dhidi ya kutokuwa Myahudi?" (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lawofmoses and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#save)

"Kwa maana wote wamefanya dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu"

Kwa sababu Mungu ni mtakatifu, yeyote aliye pamoja naye mbinguni lazima awe mkamilifu. Dhambi lolote litamhukumu mtu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#heaven and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#condemn)

Kusudi la sheria ya Musa

Kutii sheria haiwezi kumfanya mtu awe na haki kwa Mungu. Kutii sheria ya Mungu ni njia ambayo mtu anaonyesha kuwa anamwamini Mungu. Watu daima wamekuwa wenye haki kwa imani tu.

Mifano muhimu ya matamshi katika sura hii

Maswali ya uhuishaji

Mara kwa mara Paulo hutumia maswali ya uhuishaji katika sura hii. Inaonekana nia ya maswali haya ya uhuishaji ni kumfanya msomaji kuona dhambi zake ili atamtegemee Yesu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-rquestion and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#guilt)

<< | >>

Romans 3:1

Sentensi unganishi:

Paulo anatangaza faida walionazo Wayahudi kwa sababu Mungu aliwapa sheria zake.

Kisha ni faida gani aliyonayo Myahudi? Na ni manufaa gani ya tohara?

"Kisha Wayahudi hawana kufaidika na ahadi ya Mungu, ingawa Mungu aliahidi wangeweza!"

Ni kubwa

"Kuna faida nyingi"

Kwanza kabisa

Hii ina maana kwamba ama 1) "Kwanza katika utaratibu wa wakati" au 2) "Amina" (UDB) au 3) "Muhimu zaidi."

Romans 3:3

Lakini itakuwaje iwapo baadhi ya Wayahudi hawakuwa waaminifu? Je, kutoamini kwao hufanya uaminifu wa Mungu ni batili?

Paulo anatumia maswali haya na kufanya watu kufikiri. Baadhi ya Wayahudi hawakuwa waaminifu kwa Mungu, hivyo baadhi ya kuhitimisha kwamba Mungu hakutaka kutimiza ahadi yake.

Haiwezekani kamwe kuwa

Msemo huu mzito kuhusu kwamba hii inaweza kutokea. Unaweza kuwa na maelezo kama hayo katika lugha yako kwamba unaweza kutumia hapa. AT 'Hiyo haiwezekani' au 'Hakika siyo.'

Badala

"Tunapaswa kusema hili badala"

Kama ilivyokua imeandikwa

"Maandiko ya Kiyahudi wenyewe kukubaliana na ninachosema"

Romans 3:5

Lakini ikiwa uovu wetu unaonyesha haki ya Mungu, tuseme nini?

Paul ni kuweka maneno haya katika kinywa cha mtu imaginary Wayahudi anazungumza. 'Kwa sababu uovu wetu unaonyesha kuwa Mungu ni mwenye haki, nina swali'

Mungu si mwema wakati anapotoa ghadhabu yake, ni nani?

"Je, Mungu, aletaye ghadhabu juu ya watu, wasio waadilifu?" au "Hatuwezi kusema kwamba Mungu, aletaye ghadhabu, si mwema." au "Ni lazima kusema kwamba Mungu, aletaye ghadhabu, ni mwema."

Naongea kwa mujibu wa mantiki ya kibinadamu

"Ninasema hapa nini watu kwa kawaida kusema"

jinsi gani Mungu atauhukumu ulimwengu?

Paulo anatumia swali hili kuonyesha kuwa hoja dhidi ya Injili ya Kikristo ni ujinga, tangu Wayahudi wote wanaamini kwamba Mungu anaweza na kuwahukumu watu wote. AT "Na sisi wote tunajua kwamba Mungu kwa kweli kuhukumu ulimwengu!"

Romans 3:7

Lakini ikiwa kweli ya Mungu ya uongo wangu hutoa sifa tele kwa ajili yake, kwa nini ningali bado kuhukumiwa kuwa mwenye dhambi!

Hapa Paulo anafikiria mtu kuendelea kukataa Injili ya Kikristo. adui kwamba anasema, kwa sababu dhambi yake inaonyesha haki ya Mungu, basi Mungu hapaswi kutangaza kwamba yeye ni mwenye dhambi juu ya siku ya hukumu kama, kwa mfano, anamwambia uongo.

kwanini si kusema ... kufika?

Hapa Paulo anazusha swali lake mwenyewe, ili kuonyesha jinsi ujinga ni hoja za adui yake imaginary adversary. "Mimi ili kama kusema ... kuja!"

kama sisi ni waongo huripotiwa kwa kusema

"Baadhi uongo kuwaambia wengine kwamba hiki ni nini tunasema"

hukumu juu yao ni

Itakuwa sawa tu wakati Mungu analaani maadui hawa wa Paulo, kwa kusema uongo kuhusu kile Paulo amekuwa akifundisha.

Romans 3:9

Kuunganisha maelezo

Paulo anajumuisha kwamba wote wana hatia ya dhambi, hakuna walio wema, na hakuna wa kumtafuta Mungu.

Nini basi? Je, sisi kuwatetea wenyewe?

Maana inawezekana ni 1) 'Sisi Wayahudi hawapaswi kujaribu kufikiria kwenda kuepuka hukumu ya Mungu, kwa sababu tu sisi ni Wayahudi!" (UDB) au 2) "Sisi Wakristo hatujaribu kuficha mambo maovu kwamba tunafanya!'

Hapana kabisa

Maneno haya ni yenye nguvu zaidi kuliko rahisi 'hapana,' lakini si lenye nguvu "hakika si!"

Romans 3:11

Hakuna mtu ambaye anaelewa

"Hakuna mtu kweli anatambua ukweli wa Mungu"

Hakuna mtu ambaye anamtafuta Mungu

'Hakuna mtu wa dhati anaejaribu kuwa na uhusiano mwema na Mungu'

akageuka mbali

Hapa hii ina maana kuacha kufanya kitu fulani. AT "kukataliwa Mungu na mapenzi ya haki yake kwa ajili yao"

kuwa haina maana

"zimeharibika mbali kama mapenzi ya Mungu kwa ajili yao ni wasiwasi"

Romans 3:13

Wao... wao

neno 'wao' hapa linahusu "Wayahudi na Wagiriki'"ya

Makoo yao ni kama kaburi wazi

Paulo anatumia neno picha maana kwamba kila kitu watu wasemacho ni watu wabaya na machukizo

Ndimi zao zimedanganya

"Watu kusema uongo"

Vinywa vyao vimejaa laana na uchungu

"kamili" hapa ni kukua na neno "vinywa" hapa inawakilisha mawazo ya watu. AT 'Mengi ya yale watu wanasema ni hatari na maana ya kuumiza watu wengine.

Romans 3:15

Wao...wao... Watu hawa.... wao

Hii inahusisha Wayahudi na Wayunani

Miguu yao ina mbio kumwaga damu

"Wapo katika haraka ya kudhuru na kuua watu"

Uharibifu na mateso ni katika njia zao

'Kila mtu anaishi katika njia hiyo kwamba wao kwa makusudi kujaribu kuharibu wengine na kusababisha wao kuteseka'

Njia ya amani

"Njia" ni "barabara" au "njia" AT: "Jinsi ya kuishi kwa amani na wengine"

Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yao

"Kila mtu anakataa kumpa Mungu heshima anayostahili"

Romans 3:19

chochote Sheria inasema, anaongea na

'Kila kitu ambacho sheria inasema watu lazima kufanya ni kwa' au 'amri yote ambayo Musa aliandika katika sheria ni kwa ajili ya'

ili kwamba kila kinywa inaweza kuwa kimefungwa

'Hivyo kwamba hakuna mtu anauwezo wa kusema chochote halali kujitetea mwenyewe'

mwili

Hapa ina maana kwa njia ya mfano kumaanisha binadamu wote au viumbe hai wote.

kwa

Maana inawezakua ni 1) Kwa sababu hiyo" au 2) "Hii ni kwa sababu" au 3) "Badala."

kupitia sheria inakuja kutambua dhambi

"Wakati mtu anajua sheria ya Mungu, anatambua kwamba yeye si mwema bali mwenye dhambi mbele za Mungu"

Romans 3:21

Sentensi unganishi

neno "lakini" hapa linaonyesha Paulo amekamilisha utangulizi wake na sasa anaanza kufanya hatua yake kuu.

sasa

Neno 'sasa' linahusu wakati tangu Yesu alipokuja duniani.

pasipo sheria haki ya Mungu ilipatikana kujulikana

"Mungu amefanya kujulisha njia ya kuwa mwema bila kutii sheria"

Ilikuwa kushuhudiwa kwa sheria na manabii

Maneno "sheria na manabii" rejea sehemu ya andiko kwamba Musa na manabii waliandika na kusimama kwa maandiko ya Wayahudi, ambayo yameelezewa hapa kama watu ambao hutoa ushahidi mahakamani. AT "na yale ambayo Musa na manabii waliandika kuthibitisha hili."

yaani, haki ya Mungu kupitia imani katika Yesu Kristo

"Ninamaanisha kwa haki ambayo Mungu anatupa wakati tunaamini katika Yesu Kristo"

Kwa maana hakuna tofauti

"Kwa kuwa Mungu huwaona Wayahudi kwa njia hiyo hiyo huwaona Mataifa"

Romans 3:23

Wako huru kuthibitishwa kwa neema yake kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu

"Mungu anawathibitisha kwa njia ya neema yake kwa sababu Kristo Yesu amewakomboa"

Romans 3:25

kupuuza

Maana inawezeakua ni 1) kupuuza au 2) kusamehe.

Haya yote yaliyotokea kwa maandamano ya haki yake wakati huu wa sasa. Hii ilikuwa ili aweze kuthibitisha mwenyewe tu, na kuonyesha kwamba yeye anahalalisha mtu yeyote kwa sababu ya imani yake kwa Yesu

'"Alifanya hiya ili kuonyesha haki yake wakati huu wa sasa. Alionyesha kwamba yeye ni mwenye haki na mtu ambaye inahalalisha kila mtu aliye na imani katika Yesu

Romans 3:27

Kwa misingi gani? ya matendo? Hapana, lakini kwa misingi ya imani

Majibu ya Paulo ya maswali kejeli kusisitiza kwamba kila hatua yeye anayopanga ni maamuzi ya kweli. AT: "Kwa misingi gani tunaweza kujivunia kutengwa? Je, tunatengwa kwa misingi ya matendo? Hakuna, badala, ni tunatengwa kwa misingi ya imani. "

Kwa msingi gani?

"Kwa sababu gani?"

Kwa matendo?

"Tunaweza kujivunia kutengwa kwa sababu sisi tunatii sheria?"

Kwa msingi wa imani

Kwa sababu tunaamini katika Yesu

bila

"mbali na"

Romans 3:29

Au ni Mungu ni Mungu wa Wayahudi tu?

"Kama Mungu angeweza tu kuhalalisha watu ambao wanatii sheria, bila yeye kuwa ni Mungu wa Wayahudi tu?'

Romans 3:31

Sentensi unganishi

Paulo amehakikisha sheria kwa imani

Je, Twaibatilisha sheria kwa imani hiyo?

"Je, sisi kupuuza sheria kwa sababu tuna imani?"

Hata kidogo

"Bila shaka hiyo si kweli!" au "Hakika si!" (UDB). Msemo huu kutoa nguvu iwezekanavyo jibu hasi kwa uliotangulia kejeli. Unaweza kutaka kuwa na kujieleza kama hiyo katika lugha yako kwamba unaweza kutumia hapa.

sisi kutekeleza sheria

"sisi kutii sheria"

Sisi

Kiwakilishi Hii inahusu Paulo, waumini wengine, na wasomaji.

Romans 4

Warumi 04 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri huweka kila mstari wa mashairi kwenye upande wa kulia zaidi ya maandiko yote ili iwe rahisi kusoma. ULB inafanya hili kwa mistari ya 7-8 ya sura hii, ambayo ni maneno kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

Kusudi la sheria ya Musa

Paulo anaendeleza nyenzo kutoka sura ya 3. Anaelezea jinsi Abrahamu, baba wa Israeli, alivyohesabiwa haki. Hata Abrahamu hakuweza kuhesabiwa haki kwa yale aliyoyafanya. Kutii sheria ya Musa hakuwezi kumfanya mtu awe na haki na Mungu. Kutii amri za Mungu ni njia ambayo mtu anaonyesha kuwa anamwamini Mungu. Watu daima wamekuwa mwenye haki kwa imani tu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#justice and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lawofmoses and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith)

Tohara

Tohara ilikuwa muhimu kwa Waisraeli. Ilibainisha mtu kama mzao wa Abrahamu. Pia ilikuwa ishara ya agano kati ya Abrahamu na Yahweh. Hata hivyo, hakuna mtu aliyehesabiwa haki kwa kutahiriwa tu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#circumcise and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#covenant)

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Maswali ya uhuishaji

Mara kwa mara Paulo hutumia maswali ya uhuishaji katika sura hii. Inaonekana nia ya maswali haya ya uhuishaji ni kumfanya msomaji kuona dhambi zake ili atamtegemee Yesu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-rquestion and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#guilt and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

<< | >>

Romans 4:1

Sentensi unganishi

Paul anathibitisha kwamba hata katika zamani waumini walikuwa haki kwa imani na si kwa sheria.

Tutapata nini basi kusema kwamba Abrahamu baba yetu kwa jinsi ya mwili, kupatikana?

Paulo anatumia swali kupata mawazo ya msomaji na kuanza kuzungumza juu ya kitu kipya. AT 'Hivi ndivyo Ibrahimu baba yetu kimwili kupatikana.

Kwa nini andiko husema

"Kwa maana tunaweza kusoma katika maandiko"

na ikahesabiwa kwake kuwa haki

"na Mungu alimtambua Abrahamu kuwa mtu mwenye haki"

Romans 4:4

Sasa kwa ajili yake ambaye anafanya kazi, malipo ni hayahesabiwi kuwa ni neema, bali kama vile zinadaiwa

Hii ni kuelezea hali ambapo mtu ambaye anafanya kazi anatarajia kuwa atalipwa kwa kazi. Mtu huyo hakubali malipo kama zawadi ya bure au "neema."

malipo

"Mshahara" au "kulipa" au "kile chuma kwa kufanya kazi"

kile zinadaiwa

"Nini mwajiri wake anadaiwa naye"

yule ambaye amehalalishwa

"Katika Mungu, ambaye amehalalisha"

imani yake inahesabiwa kuwa haki

"Mungu anaona imani ya mtu huyo kuwa ni haki" au "Mungu anaona kuwa mtu mwenye haki kwa sababu ya imani yake"

Romans 4:6

David pia anatoa baraka juu ya mtu ambaye Mungu amemhesabia haki bila matendo

"Vile vile, Daudi aliandika kuhusu jinsi Mungu huwambariki mtu ambaye Mungu humfanya kuwa haki bila matendo"

maovu ambao ni kusamehewa ... ambao dhambi zao zimefunikwa ... yule ambaye Bwana si kuhesabu dhambi

Dhana hiyo imeelezwa kwa njia tatu tofauti. AT "ambao uovu Bwana alivyowasamehe ... ambao dhambi Bwana amezifunika ... ambao dhambi Bwana hatazihesabu."

Romans 4:9

Kisha ni baraka hii alitamka tu juu ya wote waliotahiriwa, au pia juu ya wale wasiotahiriwa?

'Je, Mungu awabariki tu wale waliotahiriwa, au pia wale wale ambao si waliotahiriwa?'

tunasema

Paulo akihutubia waumini wote Wayahudi na wa Mataifa.

Imani ilihesabiwa kwa Abraham kwa haki

"Mungu alichukuliwa imani ya Ibrahimu kuwa ni haki"

Romans 4:11

muhuri ya ile haki ya imani aliyokuwa tayari mwendawazimu wakati yeye alikuwa katika kutotahiriwa

'Ishara inayoonekana kwamba Mungu kuchukuliwa kwake mwenye haki kwa sababu alikuwa anamtumaini Mungu kabla ya kutahiriwa'

Hii ina maana kwamba haki itakuwa imehesabiwa kwao

"Ili kwamba Mungu anaweza kufikiria kuwa haki"

Romans 4:13

kwamba ahadi ilitolewa kwa Ibrahimu na wazawa wake, ahadi hii kwamba wangekuwa warithi wa Dunia

Kwamba Mungu aliahidi Ibrahimu na kizazi chake kwamba wangeweza kurithi dunia

Badala yake, ilikuwa kupitia haki wa imani

Maneno "Mungu hutoa ahadi" wanaachwa nje ya msemo huu lakini wao wanaelewa. AT "lakini Mungu alimpa ahadi kwa imani ambayo yeye aliiona kuwa ni haki."

kama wote wafuatao sheria ndio warithi

'Ikiwa ni wale ambao wanatii sheria ambayo kwamba watarithi nchi'

imani ilifanywa tupu, na ahadi ilifutwa

"Imani haina thamani na ahadi ni maana'

lakini ambapo hakuna sheria, haiwezekani kuivunja

"Lakini ambapo hakuna sheria, hakuna kitu chochote cha kuasi" au "kwa sababu kuna kitu kwa watu huasi tu ambapo kuna sheria"

Romans 4:16

Kwa sababu hii hii hutokea kwa imani, hivyo kwamba inaweza kuwa kwa neema

Hapa ni sababu sisi kupokea ahadi tunapomwamini Mungu ni hivyo kwamba inaweza kuwa hadiya

Matokeo yake, ahadi ni hakika kwa wazao wote

'Ili wazao wote wa Abrahamu waweze hakika kupokea ahadi'

wale wanaojua sheria

Hii ina maana ya Wayahudi ambao hufuata sheria ya Musa.

wale ambao ni kutoka imani ya Abrahamu

Hii ina maana ya wale ambao wana imani kubwa kama Abrahamu kabla ya kutahiriwa.

baba yetu sisi sote

Hapa neno "sisi" linawahusu Paul na ni pamoja na waumini wote Wayahudi na wasio Wayahudi katika Kristo. Ibrahimu ni babu wa kimwili wa Wayahudi, lakini yeye ni baba wa kiroho wa wale walio na imani.

kama ilivyoandikwa

Ambapo imeandikwa zinaweza kufanywa wazi. "kama ilivyoandikwa katika maandiko"

Nimekufanya wewe

neno "wewe" ni umoja na inahusu Abraham

Abrahamu alikuwa katika uwepo wa yule anaemuamini, yaani, Mungu, ambaye huwapa wafu uzima

'Ibrahimu alikuwa katika uwepo wa Mungu ambaye kuaminiwa, ambaye huwapa uzima wale waliokufa'

Romans 4:18

Licha ya hali zote za nje

maana kamili ya 'hali za nje' zinaweza kufanywa wazi. AT 'Hata ingawa ilionekana vigumu kwa yeye na watoto wake.'

Basi akawa baba wa mataifa mengi

'Na matokeo ya imani ya Ibrahimu ilikuwa ni kwamba akawa baba wa mataifa mengi.'

kulingana na kile alikuwa amesema

'Kama Mungu akamwambia Ibrahimu'

Hivyo itakuwa kizazi chako

ahadi full Mungu alimpa Ibrahimu zinaweza kufanywa wazi AT 'Utakuwa na wazawa zaidi unaweza kuhesabu.'

Yeye hakuwa dhaifu katika imani

'Aliendelea kuwa imara katika imani yake'

Abrahamu alikubali kuwa mwili wake mwenyewe alikwisha kufa-akiwa na umri wa karibu miaka mia moja. Pia alikiri hali ya kufa ya tumbo la Sara

Hapa umri wa Ibrahimu zamani na kukosa uwezo wa Sara kuwa na watoto ni ikilinganishwa na kitu ambacho ni wafu. Hii inasisitiza kuwa ilionekana vigumu kwa wao kuwa na watoto. AT 'Abraham alitambua yeye alikuwa mzee sana na Sara mkewe hakuweza kuwa na watoto.'

Romans 4:20

hakusita katika kutoamini

"Hakuwa na mashaka." AT 'agizo juu ya kutenda kwa imani.'

alikuwa imara katika imani

"Akawa na nguvu katika imani yake"

Alikuwa akijua hakika

"'Ibrahimu alikuwa na uhakika kabisa"

yeye pia alikuwa na uwezo wa kukamilisha

"Mungu alikuwa na uwezo wa kufanya"

Kwa hiyo hii ilikuwa pia kuhesabiwa kwake kama haki

"Mungu kuhesabiwa imani ya Ibrahimu kuwa ni uadilifu" au "Mungu kuchukuliwa Ibrahimu haki kwa sababu Ibrahimu aliamini yeye"

Romans 4:23

Sasa ilikuwa ni

'Sasa' limetumika hapa kuungana kuwa Ibrahimu alifanya haki kwa imani kuwasilisha siku kuhesabiwa haki muumini kwa imani katika kifo cha Kristo na ufufuo.

tu kwa faida yake

kwa Ibrahimu tu'

kwamba ikahesabiwa kwake

'Kwamba Mungu kuhesabiwa haki kwake' au 'Mungu kuchukuliwa kwake mwenye haki'

kwa ajili yetu

Neno 'sisi' inahusu Paul na ni pamoja na waumini wote katika Kristo.

Hiyo ilikuwa imeandikwa pia kwa ajili yetu, waliowekewa kuhesabiwa, sisi ambao wanaamini

"Ilikuwa pia kwa faida yetu, kwa sababu Mungu alizingatia haki yetu pia kama tunaamini"

Yeye aliyemfufua

'Mungu aliyemfufua'

Hii ni moja ambaye alitolewa kwa ajili ya makosa yetu

'Hii ni yule ambaye Mungu kukabidhiwa kwa wale waliokuwa wanamuua'

na kufufuka ili tupate kuhesabiwa haki

'Na ambaye Mungu alimrudishia uhai hivyo sisi tutafanywa sahihi na Mungu"

Romans 5

Warumi 05 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Wasomi wengi wanaona mistari ya 12-17 kama baadhi ya vifungu muhimu zaidi, lakini vigumu kuelewa, katika Maandiko. Baadhi ya ukwasi na maana yao labda imepotea wakati wa kutafsiriwa kutoka kwa jinsi Kigiriki cha awali kilikuwa.

Dhana maalum katika sura hii

Matokeo ya kuhesabiwa haki

Jinsi Paulo anavyoeleza matokeo ya kuhesabiwa haki ni sehemu muhimu ya sura hii. Matokeo haya ni pamoja na kuwa na amani na Mungu, kuwa na uwezo wa kumfikia Mungu, kuwa na uhakika juu ya kesho, kuwa na furaha wakati wa kuteseka, kuokolewa milele, na upatanisho na Mungu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#justice)

"Wote wametenda dhambi"

Wasomi wamegawanyika juu ya kile Paulo alimaanisha katika mstari wa 12: "Na kifo kilienea kwa watu wote, kwa sababu wote walitenda dhambi." Wengine wanaamini kuwa watu wote walikuwapo katika "uzao ya Adamu." Kwa hiyo, kama Adamu ni baba wa wanadamu wote, watu wote walikuwapo wakati Adamu alifanya dhambi. Wengine wanaamini kwamba Adamu alikuwa mwakilishi wa wanadamu. Kwa hiyo, alipotenda dhambi, watu wote "walianguka" kwa sababu hiyo. Ikiwa watu leo ​​walihusika au kutohusika katika dhambi ya awali ya Adamu, ni tofauti moja kati ya maoni haya. Vifungu vingine vitasaidia mtu kuamua. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#seed and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-activepassive)

Adamu wa pili

Adamu alikuwa mtu wa kwanza na "mwana" wa kwanza wa Mungu. Aliumbwa na Mungu. Alileta dhambi na kifo ulimwenguni kwa kula matunda yaliyokatazwa. Paulo anaelezea Yesu kama "Adamu wa pili" katika sura hii na mwana wa kweli wa Mungu. Yeye huleta uzima na alishinda dhambi na kifo kwa kufa kwenye msalaba. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sonofgod and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#death)

<< | >>

Romans 5:1

Kuunganishi Sentensi

Paulo anaanza kusema mambo mengi tofauti yanayotokea pindi Mungu anawathibitisha wakristo

Tangu

"Kwa sababu"

sisi...vyetu

Yote yanayotokea kwa "sisi" na "vyetu" urejea kwa wakristo wote na inapaswa kuhusisha.

kupitia Bwana wetu Yesu Kristo

"kwa sababu ya Bwana wetu Yesu Kristo"

Bwana

Hapa "Bwana" ina maanisha kwamba Yesu ni Mungu

Kupitia yeye sisi pia tuna upenyo kwa imani kufikia neema ambayo tunasimama

Paulo analinganisha wakristo kupokea neema kwa mtu aliyesimama mbele ya mfalme. "Kwa sababu ni ndani ya Yesu tuna amini, Mungu utupa neema kusimama mbele ya Mungu."

Romans 5:3

Si hivi tu

Neno "hivi" urejea kwa mawazo yaliyoelezwa ndani

Sisi...vyetu...sisi

Yote yanayotokea kwa "sisi" "vyetu" na "sisi" urejea kwa wakristo wote na inapaswa kuhusishwa

kukubalika

Neno hili "kukubalika" urejea kwa usemi wa Mungu kwamba hii ni nzuri

ujasiri kwa wakati ujao

Hii ni hakika kwamba Mungu atatimiza ahadi zake zote kwa wale wanao mwamini Kristo.

Romans 5:6

sisi

Neno "sisi" hapa urejea kwa wakristo wote na inapaswa kuhusishwa.

Romans 5:8

thibitisha

"huonyesha"

sisi...sisi

Yote yanayotokea kwa "sisi" na "sisi" urejea kwa wakristo wote na inapaswa kuhusishwa.

Zaidi ya yote, basi, sasa tumethibitishwa kwa damu yake

"Je si zaidi yeye atafanya kwetu kwa ajili yetu sasa kwamba tumelithibitishwa kwa damu yake"

kuokolewa

Hapa inamaanisha kwamba kupitia kifo cha Yesu pale msalabani, Mungu amekwisha kumsaheme na kumuokoa kwa adhabu ya jehanamu kwa ajili ya dhambi zake.

Romans 5:10

sisi...sisi

Yote yatokeayo kwa "sisi" urejea kwa wakristo wote na inapaswa kuhusishwa.

Mwana wake...maisha yake

"Mwana wa Mungu...maisha ya mwana wa Mungu"

tulikuwa tumepatanishwa kwa Mungu kupitia kifo cha mwana wake

Kifo cha mwana wa Mungu kimetupa msamaha wa milele na kutufanya sisi marafiki pamoja na Mungu, kwa wote wanaoamini katika Yesu.

Mwana

Hili ni jina muhimu kwa Yesu, Mwana wa Mungu

baada ya kuwa tumepatanishwa

"sasa basi Mungu hutuona sisi marafiki wake tena"

Romans 5:12

Sentensi unganishi:

Paulo aeleza kwa nini kifo kilitokea hata kabla ya sheria ya Mungu haijaandikwa.

kupitia mtu mmoja dhambi iliingia...kifo kiliingia kupitia dhambi

Paulo aelezea "dhambi" kama jambo hatari ambalo liliweza kuja katika ulimwengu kupitia uwazi ulio sababishwa na matendo ya "mtu mmoja" Adamu. Hii "dhambi" basi ilifanyika uwazi ambako "kifo", jambo jingine la hatari, pia lilikuja ulimwenguni.

Romans 5:14

Bila shaka

"Bado" au "Hapakuwa na kuandikwa kwa sheria kutokea wakati wa Adamu mpaka wakati wa Musa, lakini"

kifo kilitawala kutokea Adamu mpaka Musa

Paulo analinganisha kifo na mfalme. "watu waliendelea kufa kutokea wakati wa Adamu mpaka wakati wa Musa kama matokeo ya dhambi zao."

hata kwa wale hawakutenda dhambi kama kutotii kwa Adamu

"hata watu ambao dhambi zao zilikuwa tofauti na za Adamu waliendelea kufa"

yeye ni mfano wa yeye aliyepaswa kuja

Adamu alikuwa mfano wa Kristo, ambaye alijitokeza badae. Alikuwa na vitu vya kufanana naye.

Kwa kuwa kama...wengi walikufa...zaidi sana neema ya Mungu na zawadi...kuongezeka

Ni muhimu kwamba "wengi walikufa," lakini ni ya umuhimu zaidi kwamba "neema ya Mungu na zawadi" ziliongezeka

zaidi ilivyofanya neema...na zawadi...kuongezeka

"Neema... na zawadi" zilikuwa kubwa na imara kuliko makosa

Romans 5:16

Kwa kuwa zawadi si tokeo la yule aliyefanya dhambi

"zawadi si tokeo la dhambi ya Adamu"

kwa upande mmoja

"Kwa sababu ya upande mmoja"

kwa upande mmoja, hukumu ya kukataliwa ilikuja kwa sababu ya kosa la mtu mmoja. Lakini kwa upande mwingine

Kikundi cha maneno "kwa upande mmoja" na 'lakini kwa upande mwingine" utanguliza njia mbili tofauti za kufikiri kuhusu kitu fulani. "hukumu ya kukataliwa ilikuja kwa sababu ya makosa ya mtu mmoja, lakini"

baada ya makosa mengi

"baada ya dhambi za wengi"

Kosa la mmoja

Kosa la Adamu

kifo kilitawala

"kila mmoja alikufa"

maisha ya yule mmoja

maisha ya Yesu Kristo

Romans 5:18

kupitia kosa moja

"kupitia dhambi moja iliyofanywa na Adamu" au kwa sababu ya dhambi ya Adamu"

tendo moja

dhabihu ya Yesu Kristo

kutotii kwa mtu mmoja

kutotii kwa Adamu

utiifu wa mtu mmoja

utiifu wa Yesu

Romans 5:20

sheria ilikuja na

"Sheria ilikuja kwa siri"

kosa liweze kuongezeka

Hii ina maanisha vyote kwamba "watu wapate kuelewa kwa kiasi gani wamefanya dhambi" na "watu wapate kufanya dhambi zaidi."

kuongezeka

"kuongezeka"

kama dhambi utawala katika kifo

"kama dhambi ilivyosababisha kifo"

hata neema iweze kutawala kupitia haki kwa maisha ya milele kupitia Yesu Kristo Bwana wetu

"neema iliwapa watu maisha ya milele kupitia haki ya Yesu Kristo Bwana wetu"

Bwana wetu

Paulo anawajumuisha wasomaji wake na wakristo wote.

Romans 6

Warumi 06 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Paulo anaanza sura hii kwa kujibu jinsi mtu anavyoweza kupinga kitu ambacho alifundisha katika Sura ya 5. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-hypo)

Dhana maalum katika sura hii

Kinyume na Sheria

Katika sura hii, Paulo anapinga mafundisho ya kwamba Wakristo wanaweza kuishi wanavyotaka baada ya kuokolewa. Wasomi wanaita hii "uasi" au kuwa "kinyume na sheria." Kuhamasisha maisha ya kiungu, Paulo anakumbuka gharama kubwa ambayo Yesu alilipa ili Mkristo aokolewe. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#save and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#godly)

Watumishi wa dhambi

Kabla ya kumwamini Yesu, dhambi huwafanya watu kuwa watumwa. Mungu huwaachilia Wakristo kutotumikia dhambi. Wana uwezo wa kuchagua kumtumikia Kristo katika maisha yao. Paulo anaelezea kwamba wakati Wakristo wanachagua kutenda dhambii, wao huchagua kutenda kwa hiari yao. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

Matunda

Sura hii inatumia taswira ya matunda. Mfano wa matunda mara nyingi inaashiria imani ya mtu inayozalisha matendo mema katika maisha yao. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#fruit and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous)

Mifano muhimu ya matamshi katika sura hii

Maswali ya uhuishaji

Paulo anatumia maswali ya uhuishaji katika sura hii. Inaonekana nia ya maswali haya ya uhuishaji ni kumfanya msomaji kuona dhambi zake ili amtegemee Yesu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-rquestion and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#guilt and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Kifo

Paulo anatumia "kifo" kwa njia nyingi tofauti katika sura hii: kifo cha kimwili, kifo cha kiroho, dhambi inayotawala ndani ya moyo wa mwanadamu, na kumaliza kitu. Anatofautisha dhambi na kifo na maisha mapya yanayotolewa na Kristo na njia mpya Wakristo wanapaswa kuishi baada ya kuokolewa. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#death)

<< | >>

Romans 6:1

Sentensi unganishi:

Chini ya neema, Paulo anawambia wale wanaomwaminiu Yesu kuishi maisha mapya kama wafu katika dhambi na hai kwa Mungu.

Tutasema nini? Tuendelee katika dhamb ili kwamba neema iwe tele?

Paulo anategemea swali mtu mwingine atauliza kuhusiana na kile alichokiandika kuhusiana na neema

sisi...sisi

Kiwakilishi nomino "sisi" urejea kwa Paulo, wasomaji wake, na watu wengine.

tele

"kuongezeka sana"

Romans 6:4

Tulikuwa tumezikwa, basi, pamoja naye kupitia ubatizo katika kifo

Hii inalinganisha ubatizo wa mkristo katika maji pamoja na kifo cha Yesu na kuzikwa katika kaburi. Hii inasisitiza kwamba mkristo katika Kristo anagawana faida katika kifo chake, ikimaanisha dhambi haina nguvu tena juu ya mkristo.

kama vile Kristo alikuwa ameinuliwa toka mauti kupitia utukufu wa Baba, ili kwamba tuweze kutembea katika upya wa maisha.

Hii umlinganisha mkristo anakuja kwa maisha ya kiroho kwa Yesu na kurudi katika maisha ya kimwili. Maisha mapya ya kiroho humwezesha mtu kumtii Mungu. Tofasiri mbandala, "kama vile Baba alivyomleta Yesu katika uhai baada ya kufa, tuwe na maisha ya kiroho mapya na kumtii Mungu"

kuunganika pamoja naye katika kufanana kwa kifo chake...muunganike katika ufufuo wake.

"muungane pamoja naye katika kifo chake...muungane pamoja naye katika uhai baada ya kifo." "kufa pamoja naye...kurejee kwa uhai pamoja naye."

Romans 6:6

utu wa zamani ulisulubishwa pamoja naye

Hapa, Paulo arejea kwa mkristo kama mtu mmoja kabla hawajamwamini Yesu na mtu tofauti baada ya kumwamini Yesu. "Utu wa zamani" urejea kwa mtu kabla hajamwamini Yesu. Mtu huu ni mfu kiroho na dhambi umtawala. Paulo aelezea utu wetu wa zamani wa dhambi kama kufa pale msalabani pamoja na Yesu pindi tunapo mwamini Yesu. "utu wetu wa dhambi ulikuwa pale msalabani pamoja na Yesu."

utu wa zamani

Hii ina maanisha hapo awali mtu alikuwa lakina kwa sasa si hivyo. "mtu wa nyuma".

mwili wa dhambi

mwanadamu kamili wa dhambi

ili kuharibiwa

"ili afe"

hatutakuwa tena watumwa wa dhambi

Paulo analinganisha nguvu ya dhambi kuwa juu ya mtu kumiliki uongozi wa mtumwa: mtu asiye na Roho Mtakatifu mara nyingi huchagua kile kiovu. Hayuko huru kufanya yale yanayompendeza Mungu. "tusiwe watumwa tena wa dhambi" au "tusichague kufanya kile kilicho dhambi."

Yeye aliyekwisha kufa ametangazwa kuwa ana haki kulingana na dhambi

"Mungu atamtangaza haki yeyote yule aliyekufa kwa nguvu ya dhambi"

Romans 6:8

tumekwish kufa pamoja na Kristo

Ijapokuwa Kristo alikufa kimwili, hapa "kufa" urejea kwa wakristo kufa kiroho kwa nguvu ya dhambi. "tumekufa kiroho pamoja na Kristo."

Tunajua ya kuwa Kristo amekwisha inuliwa toka mauti

"Mungu alimleta Kristo katika uhai baada ya kufa"

Kifo hakimtawali tena

Hapa "kifo" kimeelezwa kama mfalme au kiongozi ambaye ana nguvu juu ya watu. "Hawezi kufa tena."

Romans 6:10

Kwa kuzingati kifo kwamba alikufa kwa dhambi, alikufa mara moja kwa yote.

Kifungu cha maneno "mara moja kwa yote" ina maanisha kumaliza kitu kabisa. Maana nzima ya hii inaweza kufanywa wazi. "Kwa maana alipokufa aliivunja nguvu ya dhambi kabisa.

Kwa njia hiyo, ninyi pia mnapaswa kufikiri

"Kwa sababu hii fikirini"

jihesabuni wenyewe

"fikirini wenyewe kama" au "kujiona wenywe kama"

kufa kwa dhambi

Hapa "dhambi" urejea kwa nguvu inayoishi ndani yetu na kutufanya sisi kutenda dhambi. "kufa kwa nguvu ya dhambi"

kufa kwa dhambi kwa upande mmoja, lakini kwa upande mwingine, kuwa hai kwa Mungu

Kikundi cha maneno "kwa upande mmoja" na "kwa upande mwingine" utanguliza njia mbili tofauti za kufikiri kuhusiana na kitu. "kufa kwa kifo lakini pia kuwa hai kwa Mungu."

kuwa hai kwa Mungu katika Kristo Yesu

"kuishi kwa kumtii Mungu kwa nguvu ya Kristo Yesu anayokupa"

Romans 6:12

Sentensi unganishi:

Paulo anatukumbusha sisi kwamba neema uongoza juu yetu, wala si sheria, sisi si watumwa wa dhambi, lakini watumwa wa Mungu.

msiache dhambi iwaongoze... Msiruhusu dhambi kuwaongoza

"Dhambi" inaelezwa kama mfalme wa mtu au bwana.

mwili wako wa kufa

Kikundi hiki cha maneno urejea kwa sehemu ya mwili wa mtu, ambayo utakufa. "wewe"

ili kusudi kwamba muweze kutii tamaa zake

Bwana. "dhambi" huitaji mwenye dhambi kutii amri za bwana kwa kufanya maovu.

Msitoe sehemu ya mwili wenu kwa dhambi kama vyombo vya udhalimu.

Hii picha ni ya mwenye dhambi anayetoa sehemu ya mwili wake kwa bwana wake au mfalme. "Msijitoe ninyi kwa dhambi ili kwamba msitende yasio faa."

lakini jitoeni kwa Mungu, kama walio hai kutoka kwenye mauti

"lakini jitoeeni ninyi kwa Mungu, kwa sababu amekwisha kuwapa ninyi maisha mapya ya kiroho"

sehemu ya miili yenu kama vyombo vya haki kwa Mungu

"acha Mungu akutumie kwa kile kimfurahisha cho yeye"

Msiruhusu dhambi kuwaongoza ninyi

"Msiache tamaa za dhambi kukuongoza kwa kile unachofanya" au "Usiruhusu wewe mwenyewe kufanya maovu unayotaka kufanya"

Kwa kuwa hamko chini ya sheria

Maana kamili inaweza kufanywa wazi. "kwa kuwa hamjafungamana na Sheria ya Musa, ambayo isingeweza kuwapa nguvu ya kuacha kufanya dhambi."

lakini chini ya neema

Maana kamili inaweza kufanywa wazi. "lakini mmefungamana na neema ya Mungu, ambayo inawapa nguvu ya kuacha kufanya dhambi."

Romans 6:15

Basi sasa? Tufanye dhambi kwa sababu hatuko chini ya sheria, lakini chini ya neema? La hasha

Paulo anatumia swali kusisitiza kwamba kuishi chini ya neema siyo sababu ya kutenda dhambi. "Hata hivyo, kwa sababu tumefungamana na neema badala ya Sheria ya Musa hakika haimaanishi tunarusiwa kufanya dhambi."

La hasha

"Hatutapenda kuona hicho kufanyika!" au "Mungu na anisaidie nisifanye hivyo!" Usemi huu uonyesha hamu mno ya nguvu kwamba hii haifanyiki. Unaweza kuhitaji kuwa na usemi kama huo katika lugha yako kwamba ungetumia hapa.

Hamjui kuwa kwake yeye mnaojitoa kama watumwa kwamba ni kwa yeye mnakuwa watumwa, ni yeye mnapaswa kumtii.

Paulo anatumia swali kumkaripia yeyote atakaye fikiri neema ya Mungu ni sababu ya kuendelea kutenda dhambi. "Mnapaswa kujua kwamba nyie ni watumwa kwa bwana mliyemchagua kumtii."

Hii ni kweli hata kama ni watumwa kwa dhambi ambayo hupelekea mauti, au watumwa wa utiifu ambayo hupelekea haki

Hapa "dhambi" na "utiifu' yameelezwa kama mabwana ambapo mtumwa atatumikia. Hii inaweza kutofasiriwa kama sentensi mpya. "Nyie sio watumwa wa dhambi, ambayo huleteleza kifo cha kiroho, au watumwa wa utiifu, ambayo husababisha Mungu awatangaze wanyofu.

Romans 6:17

Lakini ashukuriwe Mungu!

"Lakini namshukuru Mungu!"

Kwa kuwa mlikuwa watumwa wa dhambi

Hapa "dhambi" imeelezwa kama bwana ambapo mtumwa ataitumikia. Pia, "dhambi" urejea kwa nguvu inayoishi ndani yetu ambayo hutafanya sisi kuchagua kufanya kile kiovu. "Kwa kuwa mlikuwa watumwa wa nguvu ya dhambi."

lakini mmekwisha kutii toka moyoni

Hapa neno "moyo" urejea kuwa na hisia za kweli kwa kufanya kitu. "lakini hakika mlitii".

sampuli ya mafundisho yale mlipewa

Hapa "sampuli' urejea kwa njia ya kuishi ambayo hupelekea kwa unyoofu. Wakristo hubadilisha njia zao za kuishi za zamani kufanana na njia hii mpya ya kuishi ambayo viongozi wakristo huwafundisha. "mafundisho ambayo viongozi wa kikristo waliwapa ninyi."

Mme kwisha fanywa huru toka dhambi

"Kristo amewaweka huru toka kwenye nguvu ya dhambi"

watumishi wa unyoofu

"kwa sasa umtumishi wa kufanya kilicho sahihi"

Romans 6:19

Naongea kama mwanadamu

Paulo anaeleza "dhambi" na "utiifu" kama "utumwa". "Ninazungumza kuhusu utumwa kuelezea dhambi na utiifu."

kwa sababu ya udhaifu wa mwili wako

Mara nyingi Paulo utumia neno "mwili" kama kinyume cha "roho". "kwa sababu hamuelewi kwa kina mambo ya kiroho."

ilitolewa sehemu ya mwili wenu kama watumwa kwa uchafu na uovu

Hapa, "sehemu ya mwili" urejea kwa mtu kamili. "kujitoa kwenu kama watumwa kwa kila kiovu na kuto mpendeza Mungu"

toeni sehemu ya mwili wenu kama watumwa wa haki kwa ajili ya utakaso

"jitoeni kama watumwa kwa kile kilicho sahihi mbele zake Mungu ili kwamba awatenge na awape nguvu kumtumkia yeye"

Kwa wakati huo, ni tunda lipi ulipata kwa mambo ambayo sasa unayaonea aibu?

Paulo anatumia swali kusisitiza kwamba kutenda dhambi hakuleti kitu chochote kizuri. "Hakupata chochote kwa kufanya mambo hayo ambayo kwa sasa yanatia aibu."

Romans 6:22

Lakini kwa sasa umekwisha fanywa huru toka dhambi na kufanywa watumwa kwa Mungu

"Lakini sasa Kristo amekwisha waweka huru toka kwenye dhambi na amewafungamana na Mungu"

Tokeo ni uzima wa milele

"na tokeo la haya yote ni kwamba mtaishi milele pamoja na Mungu"

Kwa mshahara wa dhambi ni kifo

"Neno "mshahara" urejea kwa malipo yatolewayo kwa yeyote kwa ajili ya kazi zao. "Basi kama unatumikia dhambi, utapokea kifo cha kiroho kama malipo" au "kwa kuwa kama unaendelea kutenda dhambi, Mungu atakuhukumu na kifo cha kiroho."

lakini zawadi huru ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.

'lakini Mungu kwa uhuru hutoa uzima wa milele kwa wale walio wa Kristo Yesu Bwana wetu"

Romans 7

Warumi 07 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

"Au hujui"

Paulo anatumia maneno haya kujadili mada mpya, kwa kuunganisha maneno yanayofuata na mafundisho ya kwanza.

Dhana maalum katika sura hii

"Tumekuwa huru kutoka sheria"

Paulo anaelezea kwamba sheria ya Musa haifai tena. Ingawa hii ni kweli, kanuni zisizo na wakati kwenye sheria zinaonyesha tabia ya Mungu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lawofmoses)

Mifano muhimu ya matamshi katika sura hii

Ndoa

Maandiko ya kawaida hutumia ndoa kama mfano. Hapa Paulo anaitumia kuelezea jinsi kanisa linavyohusiana na sheria ya Musa na sasa kwake Kristo. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Mwili

Hili ni suala gumu. Kuna uwezekano kuwa "Mwili" ni mfano ya asili yetu ya dhambi. Paulo hafundishi kwamba miili yetu ya kimwili ni dhambi. Inaonekana kuwa Paulo anafundisha kwamba wakati wote Wakristo wanaishi ("katika mwili"), tutaendelea kutenda dhambi. Lakini asili yetu mpya itapigana dhidi ya asili yetu ya zamani. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#flesh and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

<< | >>

Romans 7:1

Taarifa unganishi:

Paulo anaelezea jinsi sheria inavyowatawala wale wote wanaotaka kuishi chini ya sheria.

sheria humtawala mtu muda wote anaoishi

Paulo anatoa mfano wa hili

Romans 7:2

anaitwa mzinzi

Yule ambaye "ameita" hayupo wazi, hivyo sema kwa ujumla kadiri iwezekanavyo. Mf. "Mungu atamhesabu yeye kuwa mzinzi" au "watu watamuita yeye mzinzi."

Romans 7:4

Kwa hiyo

Hii inarejea maneno haya "Kwa sababu ya jinsi sheria hufanya kazi"

tuweze kuzaa matunda kwa ajili ya Mungu

"tuweze kufanya mambo yanayompendeza Mungu"

kuzaa matunda

Hapa inamaanisha kubadilika hali ya ndani ya kiroho.

Romans 7:6

Taarifa unganishi:

Paulo anatukumbusha kwamba Mungu hatufanyi sisi kuwa watakatifu kwa njia ya sheria.

sisi

kiwakilishi hiki cha jina humaanisha Paulo na wale walioamini.

barua

"sheria ya Musa"

Romans 7:7

Tutasema nini basi?

Paulo anatambulisha mada mpya.

Isiwe hivyo kamwe

"Ndiyo hiyo si kweli!" Msemo huu unatoa kwa nguvu jibu hasi kwa swali la mtego lililotangulia. Unaweza kuwa na msemo unaofanana na huu katika lugha yako ambao unaweza kuutumia hapa.

Mimi nisingeijua dhambi kamwe, isingelikuwa ni kwa njia ya sheria...Lakini dhambi ilichukua nafasi...ikaleta kila aina ya tamaa

Paulo anaifananisha dhambi sawa na mtu ambaye anaweza kutenda.

dhambi ilichukua nafasi kupitia amri na kuleta kila aina ya tamaa ndani yangu

Wakati sheria ya Mungu inatuambi tusifanye jambo, ni kwa sababu tumeambiwa tusifanye ndio maana tunataka tufanye zaidi. "dhambi ilinikumbusha amri kutokutamani vitu viovu, na hivyo nilitamani vitu hivyo viovu zaidi kuliko mwanzo" au "kwa sababu nilitaka kutenda dhambi, wakati niliposikia ile amri ya kutotamani vitu viovu, nilivitamani"

dhambi

"hamu yangu ya kufanya dhambi"

tamaa

Neno hili linajumuisha kwa pamoja hamu ya kumiliki vitu vya wengine na tamaa mbaya ya zinaa.

pasipo sheria, dhambi imekufa

"kama kusingelikuwa na sheria, kusingelikuwa na uvunjifu wa sheria, hivyo kusingelikuwa na dhambi"

Romans 7:9

dhambi iliutawala uhai

Hii inaweza kumaanisha 1) " Nilitambua kuwa nilikuwa natenda dhambi" (UDB) 2) "Nilitamani sana kutenda dhambi."

Ile amri ambayo ingelileta uzima iligeuka kuwa mauti kwangu.

Paulo hakufa kabisa kimwili. "Mungu alinipa mimi amri ili nipate kuishi, lakini badala yake iliniua mimi."

Romans 7:11

Kwa maana dhambi ilichukua nafasi kwa ile amri na kunidanganya mimi. Kupitia ile amri, iliniua mimi.

Paulo anaielezea dhambi kama mtu anayeweza kufanya mambo 3: kuchukua nafasi, kudanganya, na kuua.

dhambi

"hamu yangu ya kutenda dhambi"

kuchukua nafasi kupitia amri

tazama ulivyotafasiri hapo awali

Romans 7:13

Taarifa unganishi:

Paul anazungumzia kuhusu vita iliyopo katika utu wake wa ndani kati ya dhambi katika utu wake wa ndani na sheria ya Mungu - kati ya dhambi na wema.

Hivyo

Paulo anatambulisha mada mpya.

kilicho kizuri

Hii inamaanisha sheria ya Mungu.

fanyika kifo kwangu

"ilisababisha mimi nife"

Isiwe hivyo kamwe

"Kwa hakika hiyo si kweli!" Msemo huu unatoa jibu hasi kwa nguvu kufuatia swali la mtego la awali. Unaweza kuwa na msemo unaofanana na huu katika lugha ambao unaweza kuutumia.

dhambi...ilileta mauti ndani yangu

Paulo anaiona dhambi kana kwamba ni mtu anayeweza kutenda.

ilileta mauti ndani yangu

"ilinitenga mimi na Mungu"

kwa njia ya amri

"kwasababu mimi sikuitii amri"

Romans 7:15

Taarifa unganishi:

Paulo anaongea kuhusu vita iliyopo kwenye utu wake wa ndani kati ya mwili wake na sheria ya Mungu - kati ya dhambi na wema.

Kwa maana nilifanyalo, kwa hakika silielewai

"Mimi sina uhakika kwanini nafanya mambo niyafanyayo"

Kwa

"Mimi sielewi kwanini nafanya niyafanyayo kwa sababu"

nisilolipenda, natenda

"Mambo ambayo najua si mema ndiyo niyafanyayo"

Lakini

"Hata hivyo"

Mimi nakubaliana na sheria

"Mimi najua kuwa sheria ya Mungu ni njema"

Romans 7:17

dhambi iishiyo ndani yangu

Paulo anaielezea dhambi kama kiumbe hai kilicho na nguvu ya kumhimiza yeye

mwili wangu

"asili ya ubinadamu wangu"

Romans 7:19

njema

"matendo mema" au "utendaji mwema"

uovu

"matendo maovu"

Romans 7:22

utu wa ndani

Sehemu ya mtu inayobaki baada ya mtu kufa

Lakini naona kanuni ya tofauti ndani ya viungo vya mwili wangu. Inapigana dhidi ya kanuni mpya kwenye akili yangu. Inanichukua mimi mateka

"Mimi naweza tu kufanya kile ambacho utu wangu wa kale unachoniambia kufanya, sio kuishi kwa njia mpya ambayo Roho ananionesha mimi"

kanuni mpya

Hii ni asili mpya ya kiroho iliyo hai.

kanuni ya tofauti katika viungo vya mwili wangu

Hii ni asili ya kale, jinsi watu walivyo wanapozaliwa.

kanuni ya dhambi iliyo ndani ya viungo vya mwili wangu

"asili yangu ya dhambi"

Romans 7:24

Ni nani atakayeniokoa na mwili huu wa mauti?

"Nataka mtu mmoja aniweke mimi huru from utawala wa kile ambacho mwili wangu hutamani" (UDB).

shukrani na ziwe kwa Mungu kwa Yesu Kristo Bwana wetu

Hili ni jibu la swali katika 7:24

Hivyo basi, kwa upande mwingine mimi mwenyewe natumikia sheria ya Mungu kwa akili zangu. Hata hivyo, kwa upande mwingine, kwa mwili mimi natumikia kanuni ya dhambi

Akili na mwili vimetumika hapa kuonesha jinsi vinavyoshabihiana aidha kwa kutumikia sheria ya Mungu au kanuni ya dhambi. Kwa akili na ufahamu mtu anaweza kuchagua kumpendeza na kumtii Mungu na kwa mwili au asili ya mwili kuitumikia dhambi. "Akili yangu inachagua kumpendeza Mungu, lakini mwili wangu huchagua kuitii dhambi."

Romans 8

Warumi 08 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Mstari wa kwanza wa sura hii ni sentensi ya kupita. Paulo anahitimisha mafundisho yake ya Sura ya 7 na anaongoza katika ya maneno ya Sura ya 8.

Baadhi ya tafsiri huweka kila mstari wa mashairi upande wa kulia zaidi kuliko maandiko yote ili iwe rahisi kusoma. ULB inafanya hii kwa mstari wa 36. Paulo ananukuu maneno haya kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

Kuishi ndani kwa Roho

Roho Mtakatifu anasemekana kuishi ndani ya mtu au ndani ya moyo wao. Ikiwa Roho yupo, hii inaashiria kwamba mtu ameokolewa. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#save)

"Hawa ni wana wa Mungu"

Yesu ni Mwana wa Mungu kwa njia ya pekee. Mungu pia anachukua Wakristo kuwa watoto wake. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sonofgod and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#adoption)

Kuchaguliwa mapema

Wasomi wengi wanamwamini Paulo katika sura hii anafundisha sana juu ya somo inayojulikana kama "kuchaguliwa mapema." Hii inahusiana na dhana ya Biblia ya "kuchagua mapema." Wengine huchukua hii ili kuonyesha kwamba Mungu, tangu kabla ya msingi wa dunia, alichagua watu wengine kuokoa milele. Wakristo wana maoni tofauti juu ya kile Biblia inafundisha juu ya suala hili. Hivyo watafsiri wanahitaji kuchukua tahadhari ya ziada wakati wa kutafsiri sura hii, hasa kuhusiana na mambo ya kusababisha. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#predestine and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#save)

Mifano muhimu ya matamshi katika sura hii

Mfano

Paulo anaeleza mafundisho yake kishairi katika mstari wa 38 na 39 kwa njia ya mfano iliyopanuliwa. Anaeleza kuwa hakuna chochote kinachoweza kumtenganisha mtu na upendo wa Mungu ndani ya Yesu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Hakuna hukumu

Kifungu hiki kinapaswa kutafsiriwa kwa uangalifu ili kuepuka kuchanganyikiwa kwa mafundisho. Watu bado wana hatia ya dhambi zao. Mungu anakataa kutenda kwa dhambi, hata baada ya kumwamini Yesu. Mungu bado anaadhibu dhambi za waumini, lakini Yesu amelipa adhabu kwa dhambi zao. Hii ndio Paulo anavyoonyesha hapa. Neno "kulaani" ina maana nyingi. Hapa Paulo anasisitiza kwamba watu ambao wanamwamini Yesu hawaadhibiwi tena milele kwa ajili ya dhambi yao kwa "kuhukumiwa kuzimu." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#guilt and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#condemn)

Mwili

Hii ni suala ngumu. "Mwili" ni mfano ya asili yetu ya dhambi. Paulo hafundishi kwamba miili yetu ya kimwili ni dhambi. Inaonekana kama Paulo anafundisha kwamba wakati wote Wakristo wanaishi ("katika mwili"), tutaendelea kutenda dhambi. Lakini asili yetu mpya itapigana dhidi ya asili yetu ya zamani. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#flesh)

<< | >>

Romans 8:1

Sentensi unganishi:

Paulo anatoa majibu kwa mapambano aliyonayo dhidi ya dhambi na wema.

kwahiyo

"kwa sababu hii" au "kwasababu ambacho nimekwisha kuwaambieni ninyi ni kweli"

kanuni...kanuni

Neno "kanuni" hapa linaelezea jinsi mambo yanavyofanya kazi kwa asili. Hii haina uhusiano wowote na taratibu zilizowekwa na watu.

Romans 8:3

Kwa maana kile ambacho sheria ilishindwa kufanya kwa sababu ilikuwa dhaifu katika mwili, Mungu alifanya

Hapa sheria inaelezwa kama mtu ambayo hakuweza kuvunja nguvu ya dhambi. "Maana sheria haikuwa na nguvu ya kutuzuia sisi kutenda dhambi, kwasababu dhambi iliyokuwa ndani yetu ilikuwa na nguvu sana. Lakini Mungu aliweza kutuzuia sisi kutenda dhambi."

katika mwili

"Kwasababu ya asili ya dhambi ya watu"

Yeye...alimtuma Mwana wake pekee kwa mfano wa mwili wa dhambi...sadaka ya dhambi...aliihukumu dhambi

Mwana wa Mungu aliiridhisha hasira takatifu ya Mungu dhidi ya dhambi kwa kuutoa mwili wake na uhai wa kibinadamu kama sadaka ya kudumu ya dhambi.

Mwana

Hili ni jina la muhimu kwa Yesu, Mwana wa Mungu.

kwa mfano wa mwili wa dhambi

"aliyeonekana kama mwanadamu mwenye dhambi mwingine yeyote"

kuwa sadaka ya dhambi

"ili kwamba afe kama sadaka kwajili ya dhambi zetu"

na alihukumu dhambi katika mwili

"na Mungu alivunja nguvu ya dhambi kupitia mwili wa Mwana wake"

mahitaji ya sheria yaweze kutimizwa kwetu

"tuweze kutimiza mahitaji ya sheria"

sisi ambao tusioenenda kwa jinsi ya mwili

"sisi ambao hatuzitii tamaa zetu za dhambi"

bali kulingana na yule Roho

"lakini wale ambao wanamtii Roho Mtakatifu"

Romans 8:6

Sentensi unganishi:

Paulo anaendelea kulinganisha miili yetu sisi kama waumini na Roho tuliye naye.

nia ya mwili...ile nia ya Roho

"jinsi ambavyo wenye dhambi hufikiri...jinsi ambavyo wale wanaomsikiliza Roho Mtakatifu hufikiri"

kifo

Hapa hii inamaanisha kutengwa kwa mtu na Mungu

Romans 8:9

katika mwili...katika Roho

Angalia maneno haya yalivyotafsiriwa hapo awali.

Roho...Roho wa Mungu...Roho wa Kristo

Haya yote yanamuelezea Roho Mtakatifu

kama ni kweli kwamba

Maneno haya hayamaanishi kwamba Paulo ana mashaka kwamba baadhi ya watu hawana Roho wa Mungu. Paulo anataka wote watambue kwamba wanaye Roho wa Mungu.

Kama Kristo yumo ndani yenu

Jinsi Kristo anavyoishi ndani ya mtu inaweza kuwekwa wazi. "Kama Kristo anaishi ndani yako kupitia Roho Mtakatifu"

kwa upande mwingine, mwili umekufa kwa mambo ya dhambi, lakini kwa upande mwingine

Kipande cha sentensi "kwa upande mwingine" na "lakini kwa upande mwingine" huonesha njia mbili za namna ya kufikiri kuhusu jambo fulani. "mwili umekufa katika mambo ya dhambi, lakini"

mwili umekufa kwa mambo ya dhambi

Uwezekano wa maana hizi mwili 1) mtu amekufa kiroho katika nguvu ya dhambi au 2) bado mwili wa nyama utakufa kwasababu ya dhambi.

roho ipo hai kwa mambo ya haki

maana yake yaweza kuwa 1) mtu yupo hai kiroho, Mungu amempa nguvu kufanya yaliyo sahihi au 2) Mungu atamrejesha mtu uzimani baada ya kufa kwasababu Mungu ni mwenye haki na huwapa walioamini uzima wa milele.

Romans 8:11

kama roho...anaishi ndani yenu

Paulo anaamini kuwa Roho Mtakatifu anaishi ndani ya wasomaji wake. "Kwa kuwa Roho...anaishi ndani yenu"

ya yule aliyemfufua

"ya Mungu, aliyemfufua"

fufuliwa

Hapa hii imaanisha kumfanya mtu alikufa kuwa hai tena.

mwili wa kibinadamu

"mwili wa nyama" au "miili, ambayo siku moja itakufa"

Romans 8:12

Hivyo basi

"Kwasababu yale niliyokwisha kuwaambia ni kweli"

ndugu

"waumini wenzangu"

sisi tu wadeni

Paulo analinganisha utii kama kulipa deni. "tunahitaji kutii"

lakini sio kwa mwili kuishi kulingana na mwili

"lakini sisi si wadeni wa mwili, na sisi hatupaswi kuzitii tamaa zetu za dhambi"

Kwa maana mkiishi kwa jinsi ya mwili

"Kwasababu mkiishi tu kwa kupendeza tamaa zenu za dhambi"

mko karibu kufa

"hakika mtatengwa na Mungu"

lakini ikiwa kwa Roho mnayafisha matendo ya mwili

"Lakini ikiwa kwa nguvu ya Roho Mtakatifu mnaacha kuzitii tamaa zenu za dhambi"

Romans 8:14

Maana kama ambavyo wengi wanaongozwa na Roho wa Mungu

"Kwa watu wote ambao Roho wa Mungu anawaongoza"

wana wa Mungu

Hapa hii inamaanisha walioamini wote katika Yesu na mara nyingi hutafsiriwa kama "watoto wa Mungu."

Kwa kuwa hamkupokea roho ya utumwa tena hata muogope

"Kwa kuwa Mungu hakuwapa ninyi roho inayowanya ninyi kuwa watumwa tena wa nguvu ya dhambi na hofu ya hukumu ya Mungu"

ambayo kwayo tunalia

"inayotufanya sisi tulie"

Abba, Baba

"Abba" ni "Baba" kwa lugha ya Kiaramaiki.

Romans 8:16

warithi wa Mungu kwa upande mmoja. Na warithi pamoja na Kristo kwa upande mwingine

Vipande vya sentensi "kwa upande mmoja" na "kwa upande mwingine" hutambulisha njia mbili tofauti za kufikiri kuhusu jambo fulani. "warithi wa Mungu na pia warithi pamoja na Kristo"

kwamba pia tuweze kupewa utukufu pamoja naye

"kwamba atatutukuza sisi pamoja naye"

Romans 8:18

Sentensi unganishi:

Paulo anatukumbusha kuwa miili yetu itabadilishwa katika ukombozi wa miili

Kwa

Hii inasisitiza "Mimi nafikiri." Haimaanishi "kwasababu"

Mimi nafikiri kwamba...haistahili kulinganishwa na

"Mimi sifikiri kwamba...yanastahili kulinganishwa na"

itafunuliwa

"Mungu atayafunua" au "Mungu atafanya yajulikane"

viumbe vinatazamia kwa shauku

Kila kitu ambacho Mungu ameumba kimeelezwa kama mtu anayengoja kitu kwa shauku.

kwa kufunuliwa kwa wana wa Mungu

"kwa wakati ambao Mungu atawafunua watoto wake"

wana wa Mungu

Hapa hii imaanisha walioamini wote katika Yesu na mara nyingi imetafsiriwa kama "watoto wa Mungu"

Romans 8:20

Kwa maana uumbaji ulitiishwa chini ya ubatili

"Kwa maana Mungu alisababisha kile alichokiumba kisiweze kufikia lengo ambalo alilolikusudia"

sio kwa mapenzi yake, bali yake yeye aliyevitiisha

Hapa "uumbaji" umeelezwa kama mtu ambaye anaweza kutamani. "sio kwa sababu kwamba hiki ndicho vitu vilivyoumbwa vilihitaji, bali kwasababu ndicho ambacho Mungu alihitaji"

ni katika tumaini kwamba uumbaji wenyewe utawekwa huru

"Kwasababu Mungu alijua kwamba atauokoa uumbaji."

kutoka utumwa hadi uharibifu

Paulo anavilinganisha vitu vyote katika uumbaji na watumwa na "uharibifu" wao. "kutoka kuoza na kufa"

kwenye uhuru wa utukufu wa wana wa Mungu

"na atawaweka huru atakapowapa heshima watoto wake"

Kwa maana twajua ya kuwa uumbaji nao pia unaugua na kuteseka kwa uchungu pamoja hata sasa

Uumbaji unalinganisha na mwanamke anavyougua wakati wa kuzaa mtoto. "Kwa maana twajua ya kuwa kila kitu ambacho Mungu amekiumba kinataka kuwa huru na huugua kama mwanamke anayezaa"

Romans 8:23

tulio na malimbuko ya Roho

Paulo analinganisha jinsi walioamini wanavyopokea Roho Mtakatifu sawa na malimbuko na mboga za masika zinavyokua. Hii inasisitiza kwamba Roho Mtakatifu ni mwanzo tu wa mambo ambayo Mungu atawapa walioamini.

kusubiri kufanywa wana, ukombozi wa miili yetu

"kusubiri wakati tutakapokuwa washiriki halisi wa familia ya Mungu na atakapookoa miili yetu kutoka katika kuharibika na mauti"

Kwa maana ni kwa taraja hili tuliokolewa

"Kwa maana Mungu alituokowa kwasababu tulikuwa na imani naye"

Lakini tunachotarajia kitatokea bado hakijaonekana, kwa maana ni nani atarajiaye kile akionacho tayari?

Paulo anatumia swali kuwasaidia wasikiliaji wake kuelewa maana ya "kujiamini."

Romans 8:26

Sentensi unganishi:

Ingawa Paulo amekuwa akisisitiza kwamba kuna mapambano ndani ya walioamini kati ya mwili na Roho, anathibitisha kuwa Roho anatusaidia sisi.

kuugua kusikoweza kutamkwa

"kuugua ambako hakuwezi kuelezewa kwa maneno"

Romans 8:28

Sentensi unganishi

Paulo anawakumbusha walioamini kwamba hakuna kinachoweza kuwatenganisha na upendo wa Mungu.

kwa wale wote walioitwa

"kwa wale wote ambao Mungu aliwachagua"

wote aliowajua tangu asili

"wote ambao aliwajua hata kabla ya kuwaumba"

Yeye pia aliwachagua tangu asili

"yeye pia aliufanya mwisho wake" au "yeye pia aliupanga tangu awali"

wafananishwe na sura ya Mwana wake

Mungu alipanga kabla ya kuanza kwa uumbaji kuwakuza wale wamwaminio Yesu, Mwana wa Mungu, kuwa watu wafananao na Yesu. "kwamba angewabadilisha wawe kama Mwana wake."

Mwana

Hili ni jina la muhimu la Yesu, Mwana wa Mungu.

kwamba awe mzaliwa wa kwanza

"ilikwamba Mwana wake awe mzaliwa wa kwanza"

kati ya ndugu wengi

"miongoni mwa akina kaka na dada wengi ambao ni wa familia ya Mungu"

Wale ambao aliwachagua tangu asili

"Wale ambao Mungu aliwapangia kabla"

hao pia akawatukuza

Neno "kutukuzwa" ni nyakati zilizopita kuonesha msisitizo kwamba hili litatokea hakika.

Romans 8:31

Tuseme nini basi juu ya mambo haya? Mungu akiwa upande wetu, ni nani aliye juu yetu?

Paulo anatumia swali kusisitiza wazo kuu kwa yale aliyoyasema hapo awali. "Hiki ndicho tunachopaswa kujua kutoka haya yote: kwa Mungu anatusaidia sisi, hakuna awezaye kutushinda sisi"

Yeye asiyemwachilia mwana wake mwenyewe

Mungu Baba alimtuma Mwana wa Mungu, Yesu Kristo, msalabani kama sadaka takatifu isiyo na mwisho ya muhimu kumridhisha asili ya milele ya Mungu dhidi ya dhambi ya wanadamu.

bali alimtoa

"lakini alimkabidhi kwa adui"

atakosaje kutukirimia na mambo yote pamoja naye?

Paulo anatumia swali kwa ajili ya msisitizo. "Yeye kwa hakika na kwa uhuru atatupatia vitu vyote"

Romans 8:33

Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki

Paulo anatumia swali kusisitiza. "Hakuna mtu anayeweza kutuhukumu sisi kwa Mungu kwasababu ndiye atupatanishaye naye."

Ni nani atakayewahukumia adhabu?

Paulo anatumia swali kusisitiza. Hatarajii jibu kutoka kwao. "Hakuna atakayetuhukumu"

na zaidi ya hayo, yeye pia alifufuliwa

"ambaye muhimu sana Mungu alimfufua kutoka wafu" au "ambaye kwa muhimu zaidi aliurudia uzima"

Romans 8:35

Ni nani atakayetutenga sisi na upendo wa Kristo?

Swali hili linaonekana kuuliza kuhusu mtu, lakini jibu lifuatalo linazuia matukio, sio watu. Hivyo Paulo labda anaongea kuhusu matukio kama vile na watu

Dhiki, au shida, au mateso, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga?

"Haiwezekani hata kama mtu yeyote atatusababishia shida, atatuumiza, atachukua mavazi yetu au chakula, au hata kutuua."

Dhiki, au shida

Maneno haya yote yana maana moja.

Kwa faida yako

Hapa "yako" ipo katika umoja na inamaanisha Mungu.

tunauawa mchana kutwa

Hapa "sisi" inarejea kwa yule aliyeandika kifungu hiki cha Maandiko na inajumuisha wale wote wanaomtii Mungu. Maneno "mchana kutwa" ni maneno yaliyoongezwa kusisitiza kiwango cha hatari waliyomo. Paulo anatumia sehemu hii ya Maandiko kuonesha kwamba wote walio wa Mungu watarajie nyakati ngumu. "adui zetu wanaendelea kututafuta watuue"

Sisi tulihesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa

Hii inalinganisha kati ya watu wanaouawa kwasababu ya utii wao kwa Mungu na wanyama. "Maisha yetu hayakuwa na thamani kwao kuliko kondoo wanaowaua"

Romans 8:37

sisi ni zaidi ya washindi

"tunao ushindi kamili"

katika yeye aliyetupenda

Aina ya upendo ambao Yesu alituonesha unaweza kuwekwa wazi. "kwasababu ya Yesu, aliyetupenda sana alikuwa tayari kufa kwa ajili yetu."

Mimi nimekwisha shawishika

"Nimeshawishiwa" au "Nina ujasiri"

mamlaka

Maana inaweza kuwa 1) mapepo (UDB) au 2) wafalme na watawala wa kibinadamu.

wala nguvu

Maana inaweza kuwa 1) viumbe vya kiroho vyenye nguvu au 2) wanadamu wenye nguvu.

Romans 9

Warumi 09 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Katika sura hii, Paulo anaacha mafundisho ya kwanza. Katika Sura ya 9-11, anazingatia taifa la Israeli.

Baadhi ya tafsiri huweka kila mstari wa mashairi upande wa kulia zaidi kuliko maandiko yote ili iwe rahisi kusoma. ULB hufanya hivi kwa mistari 25-29 na 33 ya sura hii. Paulo ananukuu maneno haya yote kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

Mwili

Paulo anatumia neno "mwili" katika sura hii kutaja Waisraeli, wazao wa Abrahamu kupitia Yakobo, ambaye Mungu alimwita Israeli. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#flesh)

Katika sura nyingine, Paulo anatumia neno "ndugu" kumaanisha Wakristo wenzake. Hata hivyo, katika sura hii, anatumia "ndugu zangu" kumaanisha jamaa zake Waisraeli.

Paulo anaelezea wale wanaomwamini Yesu kama "watoto wa Mungu" na "watoto wa ahadi."

Kuchaguliwa mapema

Wasomi wengi wanaamini kama Paulo katika sura hii anafundisha sana juu ya somo inayojulikana kama "kuchaguliwa mapema." Hii inahusiana na dhana ya Biblia ya "kuchagua mapema." Wengine huchukua hii ili kuonyesha kwamba Mungu, tangu kabla ya msingi wa dunia, alichagua watu wengine kuokoa milele. Wakristo wana maoni tofauti juu ya kile Biblia inafundisha juu ya suala hili. Hivyo watafsiri wanahitaji kuchukua tahadhari ya ziada wakati wa kutafsiri sura hii, hasa kuhusiana na mambo ya kusababisha. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#predestine and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#save)

Mifano muhimu y matamshi katika sura hii

Jiwe la kikwazo

Paulo anaelezea kwamba ingawa Wayunanai wamoja wamempokea Yesu kama mwokozi wao kwa kumwamini, Wayahudi wengi walikuwa wanajaribu kupata wokovu wao kwa kufanya kazi wenyewe na hivyo wakamkataa Yesu. Paulo, akinukuu Agano la Kale, anaelezea Yesu kama jiwe ambalo Wayahudi wanakumbwa wakati wa kutembea. "Jiwe la kuwakwaza" huwafanya "kuanguka." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Sio kila mtu wa Israeli ambaye ni wa Israeli"

Paulo anatumia neno "Israeli" katika aya hii kwa maana mbili tofauti. "Waisraeli" ya kwanza inamaanisha wazao wa Abrahamu kupitia Yakobo. "Waisraeli" ya pili ina maana wale ambao ni watu wa Mungu kupitia imani. UDB inaonyesha hii.

<< | >>

Romans 9:1

Sentensi unganishi:

Paul anaeleza kuhusiana na shauku yake kwamba watu wa taifa la Israeli wangeokolewa, kisha anasisitiza njia tofauti ambazo Mungu ameandaa kwa kuamini.

na dhamiri yangu hushuhudia ndani yangu katika Roho Mtakatifu.

Njia mbadala ya utofasiri: "Roho Mtakatifu huongoza dhamiri yangu na kuhakiki nisemacho"

kwa kuwa kwangu mimi kuna huzuni kubwa na maumivu yasiyo koma ndani ya moyo wangu.

Kama nafsi ya Paul ambayo inahuzunika inahitajika kusemwa, tumia tofasiri nyingine: " Ninakuambia kwamba ninahuzunika kwa wingi na kwa undani."

huzuni kubwa na maumivu yasiyo koma

Hii misemo miwili inamaanisha haswa maana ile ile. Paulo anatumia kwa pamoja kwa kusisitiza ni kwa namna gani hisia zake zilivyo.

Romans 9:3

Kwamba ningetamani mimi mwenyewe kulaaniwa na kutengwa mbali na Kristo kwa ajili ya ndugu zangu, wale wa jamii yangu katika mwili.

Mimi binafsi ningekuwa tayari kumwacha Mungu anilaani mimi na, kuniweka mimi mbali na Kristo milele kama hiyo ingewasaidia ndugu zangu waisraeli, watu wa kundi langu, kumwamini Kristo."

Wao ni waisraeli

"Wao, kama mimi, ni waisraeli. Mungu aliwachagua wao kuwa uzao wa Yakobo"

Wao ni watangulizi ambako Kristo amekuja kwa heshima ya mwili.

Kristo amekuja kwa mwili kama mzao kutoka kwa watungulizi wao.

Romans 9:6

Sentensi unganishi:

Paulo anasisitiza kwamba wale waliozaliwa katika familia ya Israeli wanaweza kwa kweli kuwa sehemu ya Israeli kupitia imani.

Lakini si kwamba ahadi za Mungu zimeshindwa kutimia

"Lakini Mungu hajashindwa kutimiza ahadi zake"

Kwa kuwa si kila mtu aliye Israeli ni mwiisraeli halisi.

Mungu hakuzifanya ahadi zake kwa uzao wote kimwili wa israeli (au Yakobo), lakini kwa uzao wake wa kiroho, kwamba, wale walio na imani katika Yesu.

Si wote ni uzao wa Ibrahihim ni watoto wake hilisi.

"Wala si kwamba ni wana wa Mungu kwa sababu ni wazao wa Ibrahimu"

Romans 9:8

watoto wa mwili

Hii inarejesha kwa watu ambao ni uzao wa Ibrahimu kwa mwili.

Watoto wa Mungu

Hii inarejesha kwa watu ambao ni uzao wa kiroho walio na imani ndani ya Yesu.

watoto wa ahadi

Hii inarejesha kwa watu watakaoridhi ahadi ya Mungu.

Sara atapewa mtoto

"Nitampa Sara mwana"

Romans 9:10

baba yetu Isaka...sasa hivi

Katika utamaduni unaweza kuhitaji kuweka 9:11 baada ya 9:12. Tofasiri mbadala: "baba yetu Isaka, ilisemwa kwake, ' Mkubwa atamtumikia mdogo.' Sasa watoto walikuwa bado hawajazaliwa...kwa sababu ya yeye aitae. Ni sasa"

baba yetu

Isaka alikuwa mtangulizi wa Paulo na wakristo wayahudi katika Rumi.

kubeba mimba

"alibeba ujauzito"

kwa kuwa walikuwa bado hawajazaliwa na hakuwa amefanya lolote zuri au baya

"kabla watoto hawajazaliwa na hakuwa amefanya lolote zuri au baya"

ili kwamba kusudi la Mungu kulingana na uchaguzi lisamame

"ili kwamba Mungu anachotaka kifanyike kulingana na uchaguzi wake kifanyike"

kwa kuwa watoto walikuwa bado hawajazaliwa

"kabla watoto hawajazaliwa"

na hakuwa amefanya lolote zuri au baya

"si kwa sababu ya lolote walikuwa wamefanya"

kwa sababu yake

kwa sababu ya Mungu

ilikuwa imesemwa kwake, "Mkubwa atamtumikia mdogo".

Mungu alisema kwa Rebeka, 'Mwana mkubwa atamtumikia mwana mdogo"

Nilimpenda Yakobo, lakini nilimchukia Esau

Mungu alimchukia Esau pekee katika ulinganisho wa kiasi gani alivyompenda Yakobo.

Romans 9:14

Basi tena tutasema nini?

Paulo anatumia swali kusahihisha hitimisho kwamba Mungu si dhalimu.

La hasha

"Hilo haliwezekani!" au bila shaka!" Usemi hii kwa nguvu hukanusha kwamba hii ingewezekana kufanyika. Unaweza kuwa na usemi wa kufanana katika lugha yako kwamba ungeweza kutumia hapa.

Kwa kuwa anasema kwa Musa

"Kwa kuwa Mungu anasema kwa Musa"

Si kwa sababu yeye anataka, wala kwa sababu ya yeye akimbiae

"Si kwa sababu ya wale watu hupenda au kwa sababu wanajaribu kwa nguvu"

wala si kwa sababu ya yeye akimbiae

Paul anamlinganisha mtu anayekimbia mbio kwa mtu ambaye anajitahidi kwa nguvu kufikia lengo.

Romans 9:17

Kwa kuwa maandiko husema

Hapa andiko limefanyika nafsi hai kama Mungu anazungumza na Farao. "Maandiko hutunza kumbukumbu kwa Mungu kusema"

Mimi...changu

Mungu anarejesha kwake mwenyewe.

wewe

umoja

na ili kwamba jina langu litangazwe katika inchi yote.

"na kwamba watu waweze kulitangaza jina langu katika inchi yote"

na yeye ambaye apendaye, humfanya kuwa mgumu wa moyo.

Mungu humfanya mgumu wa moyo yule apandaye kumfanya.

Romans 9:19

Kisha utasema kwangu

Paulo anazugumza hukumu ya mafundisho yake kama vile alikuwa anaongea na mtu mmoja. Unaweza kuhitajia kutumia wingi hapa.

yeye...yake

Maneno 'yeye' na 'yake' hapa yanarejesha kwa Mungu

hivi kilichofinyangwa cha weza sema... matumizi ya kila siku?

Paulo anatumia haki ya mfinyazi kutengeneza aina yoyote ya chombo anachotaka kutokana na udongo kama mfano wa haki ya muumbaji kufanya chochote anachotaka na umbaji wake.

kwanini ulinifanya hivi mimi

Neno "wewe" hapa urejea kwa Mungu.

Romans 9:22

yeye...yake

Maneno "yeye" na "yake" urejea kwa Mungu.

vyombo vya gadhabu...vyombo vya rehema

"watu wanaostahili gadhabu...watu wanaostahil rehema"

wingi wa utukufu wake

"utukufu wake, ambao ni dhamani kubwa"

ambao alikwisha kuandaa kwa ajili ya utukufu.

"ambao alikwisha kuaanda mbele ya wakati kutoa utukufu"

pia kwa ajili yetu

Neno "yetu" hapa urejea kwa Paulo na wakristo wenzake.

kuitwa

Hapa hii ina maanisha Mungu amewateua au kuchagua watu kuwa watoto wake, kuwa watumishi wake nd watangazaji wa ujumbe wake wa wokovu kupitia Yesu.

Romans 9:25

Sentensi unganishi:

Kaitka sehemu hii Paul anaeleza namna kuto amini kwa waisraeli kama taifa kulisemwa mbele ya wakati na nabii Hosea.

Kama asemavyo katika Hosea

"Kama Mungu asemavyo pia katika kitabu cha Hosea aliandika"

Hosea

Hosea alikuwa nabii

Nitawaita watu wangu ambao hawakuwa watu wangu

" Nitawachagua watu ambao hawakuwa watu wangu kuwa watu wangu"

mpendwa wake ambaye hakuwa amependwa

"Nitamchagua yeye ambaye siku mpenda kuwa mmoja wa yule ninaye mpenda"

wana wa Mungu aliye hai

Neno "hai" linaweza kurejea kwa kigezo kwamba Mungu ni pekee wa "kweli", na siyo kama sanamu za uongo. Tofasiri mbadala: "watoto wa Mungu wa kweli"

Romans 9:27

hulia

"huita"

kama mchanga wa bahari

"ni zaidi kuhesabu"

wataokolewa

Kuokolewa imetumika katika maana ya kiroho. Kama mtu "ameokolewa", ina maanisha kwamba kupitia kuamini kifo cha Yesu pale msalabani, Mungu amekwisha msahehe na kumkomboa yeye kutoka katika kuhukumiwa kwa dhambi yake.

neno

Hii inarejea kwa kila kitu Mungu alichosema au kuamuru.

yetu...sisi

Hapa maneno "yetu" na "sisi" urejea kwa Isaya na kuwajumuisha waisraeli

tungekuwa kama Sodoma, na tumefanywa kama Gomora

Unaweza kufanya kwa uwazi namna waisraeli wangekuwa kama Sodoma na Gomora. Tofasiri mbadala: "tungekuwa wote tumeteketezwa, kama miji ya Sodoma na Gomora ilivyoteketezwa.

Romans 9:30

Tutasema nini basi?

Tofasiri mbadala: "Hivi ndivyo tunapaswa kusema"

Kwamba mataifa

Tofasiri mbadala: "Tutasema kwamba wa mataifa"

ambao hawakuitafuta haki

"ambao hawakujaribu kumfurahisha Mungu"

hawakuweza kuifikia

"hawakuweza kuipata haki kwa kuifata sheria"

Romans 9:32

Kwani si hivyo?

"Kwanini hawakuweza kuifikia haki?"

kwa matendo

"kwa kujaribu kufanya mambo ambayo yangemfurahisha Mungu" au "kwa kuifata sheria"

jiwe la kujikwaa

"jiwe ambalo watu wanajikwaa"

kama ilivyo kwisha andikwa

"kama Isaya nabii aliandika"

amini ndani yake

Kwa sababu jiwe husimama kwa ajili ya mtu, unaweza kuhitaji kutofasiri "amini katika yeye"

Romans 10

Warumi 10 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri zinaweka nukuu za nathari kutoka Agano la Kale upande wa kulia zaidi wa ukurasa kushinda maandiko yote. ULB inafanya hivi kwa maneno yaliyotajwa katika mstari wa 8.

Baadhi ya tafsiri huweka kila mstari wa mashairi upande wa kulia zaidi kuliko maandiko yote ili iwe rahisi kusoma. ULB inafanya hivi kwa mistari 18-20 ya sura hii, ambayo ni maneno kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

Haki ya Mungu

Paulo anafundisha hapa kwamba ingawa Wayahudi wengi walijaribu kuwa wenye haki, hawakufanikiwa. Hatuwezi kupata haki ya Mungu kwa kazi yetu mwenyewe. Mungu anatupa haki ya Yesu tunapomwamini. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith)

Mifano muhimu ya matamshi katika sura hii

Maswali ya uhuishaji

Paulo anatumia maswali mengi ya uhuishaji katika sura hii. Anafanya hivyo kuwashawishi wasomaji wake kwamba Mungu hawaokoi watu wa Kiebrania pekee, hivyo Wakristo lazima wawe tayari kwenda kuhubiri Injili kwa ulimwengu wote. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-rquestion and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#save)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Nitawachochea wivu kwa kile ambacho si taifa"

Paulo anatumia unabii huu kuelezea kwamba Mungu atatumia kanisa kuwafanya watu wa Kiebrania kuwa na wivu. Hii ni ili wamtafute Mungu na kuamini Injili. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#prophet and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#jealous and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

<< | >>

Romans 10:1

Sentensi unganishi:

Paulo anaendelea na wazo lake kwa waisraeli kuamini lakini akisisitiza kwamba wale walio wayahudi na yoyote yule anaweza kuokolewa kwa imani katika Yesu.

Ndugu

Hapa ina maanisha wakristo wenzetu, ikijumuisha wote wanuame na wanawake.

shauku ya moyo wangu

"shauku yangu kuu"

ni kwa ajili yao, kwa ajili ya wokovu wao

"ni Mungu atakaye waokoa wayahudi"

Romans 10:4

Kwa kuwa Kristo ni hitimisho la sheria

"Kwa kuwa Kristo kwa ukamilifu alitimiliza sheria"

kwa kuwa haki ipo kwa yoyote ambaye huamini.

"ili kwamba aweze kumfanya kila moja aaminie katika yeye kuwa sawa mbele yake Mungu"

uamini

Hapa ina maanisha kuamini kitu ni kukubali au kusadiki kuwa ni kweli.

haki inayo kuja kutokana na sheria

"namna gani sheria humfanya kuwa sawa mbele zake Mungu"

Mtu ambaye hufanya haki ya sheria ataishi kwa haki hii

"Mtu ambaye kwa ukamilifu utii sheria ataishi kwa sababu sheria itamfanya yeye kuwa sawa mbele ya Mungu"

ataishi

Hii inaweza kurejea kwa 1) uzima wa milele au 2)maisha ya dunia katika ushirika pamoja na Mungu.

Romans 10:6

Lakini haki inayotokana na imani husema hivi

Hapa "haki" imeelezwa kama mtu ambaye anaweza kuongea. "Lakini Musa anaandika hivi kuhusiana na namba imani humfanya mtu sawa mbele za Mungu"

Usiseme ndani ya moyo wako

Musa alikuwa anaongea na watu kama vile walikuwa ni mtu mmoja. "Usiseme kwako mwenyewe"

Nani atakayepaa kwenda mbinguni?

Musa anatumia swali kufundisha wasikiizaji wake. Maelekezo yake ya awali, "Usiseme" huitaji jibu hasi kwa swali hili. "Hakuna mmoja asijaribu kwenda juu mbinguni"

hii ni kwamba, kumleta Kristo chini

"ili kusudi kwamba wamlete Kristo chini ya inchi"

Nani atakaye shuka katika shimo kubwa

Musa anatumia swali kuwafundisha wasikilizaji wake. Maelekezo yake ya awali, "Usiseme" huitaji jibu hasi kwa swali hili. "hakuna mmoja ajaribu kwenda chini na kuingia eneo ambao roho za watu waliokufa wapo"

hii ni, kumleta Kristo juu kutoka kwa wafu

" ili kusudi kwamba waweze kumleta Kristo kutoka kwa wafu."

kufa

Hapa ina maanisha pale mwili wa mtu huacha kuishi.

Romans 10:8

Lakini inasema nini?

Neno "ina" urejea kwa "haki"

Neno liko karibu nawe

"Ujumbe uko wapi"

katika mdomo wako

Neno "mdomo" urejea kwa kile mtu husema. Tofasiri mbadala: "kiko katika kile usemacho"

na katika moyo wako

Neno "moyo" urejea kwa akili ya mty au kile ufikiria. Tofasiri mbandala: "na kiko katika kile unachofikiri"

kama kwa mdomo wako unatambua Yesu kuwa Bwana

'kama unakiri kwamba Yesu ni Bwana"

amini katika moyo wako

"kubali kuwa ni kweli"

alimfufua yeye kutoka kwenye mauti

Hapa ina maanisha kwamba Mungu alimsababisha Yesu kuwa hai tena

utaokolewa

"Mungu atakuokoa"

Kwa kuwa kwa moyo mtu huamini kwa haki, na kwa kinywa hukiri wokovu

"Ni kwa akili kwamba mtu husadiki na kuwa mbele za Mungu, na ni kwa kinywa mtu hukiri na Mungu umuokoa"

Romans 10:11

Yeyote ambaye anamwamini yeye hatatahayarika

"Yeyote asiye amini atatayarika." Hasi hapo imetumiwa kwa usisitizo. "Mungu atamheshimu ambaye anamwamini."

hakuna tofauti kati ya Myahudi na Myunani

"Kwa njia hii, Mungu huwaona Wayahudi na wasio wayahudi sawa"

na yeye ni tajiri kwa wale wote wamwitao

"na uwabariki kwa wingi wote wamwaminio"

Kwa kila aliitae jina la Bwana ataokolewa

Neno "jina" urejea kwa Yesu. " Bwana atamuokoa kila amtegemeae."

Romans 10:14

Basi watawezaje kumwita yeye wasiye mwamini?

Paulo anatumia swali kusisitiza umuhimu wa kupeleka habari njema za Kristo kwa wale ambao hawajasikia. Neno "wale" urejea kwa wale ambao si wa Mungu. "Wale ambao hawamwamini Mungu hawawezi kumwita yeye"

Na watawezaje kuamini katika yeye ambapo hawajamsikia?

Paulo utumia swali jingine kwa sababu ile ile. "Na hawawezi kuamini katika kama hawajasikia ujumbe wake" au "Na hawawezi kuamini katika yeye kama hawajasikia ujumbe kuhusiana na yeye."

kuamini katika

Hapa ina maanisha kukiri kwamba kile mtu alichosema ni kweli.

Na watawezaje kusikia pasipo mhubiri?

Paulo anatumia swali jingine kwa sababu ile ile. "Na hawawezi ujumbe kama hakuna mtu wa kuwambia"

Na watawezaje kuhubiri, mpaka watumwe?

Paulo anatumia swali jingine kwa sababu ile ile. Neno "wale" urejea kwa wale wa Mungu. "Na hawawezi kuwaambia watu wengine ujumbe mpaka mtu awatume"

Ni mzuri miguu ya wale wanaotangaza habari njema za mambo mazuri

Paulo anatumia "miguu" kuwakilisha wale wanaosafiri na kuleta ujumbe kwa wale amba hawajasikia. "Inafurahisha pindi waleta ujumbe huja na kutuambia habari njema."

Romans 10:16

Lakini wote hawakusikiliza

"Lakini si Wayahudi wote walisikiliza'

Bwana, nani ambaye ameamini ujumbe wetu?

Paulo anatumia swali hili kusisitia kwamba Isaya alitabiri katika Maandiko kwamba Wayahudi wengi hawataamini katika Yesu. "Bwana, wengi wao hawaamini ujumbe wetu"

ujumbe wetu

hapa, "wetu" urejea kwa Mungu na Isaya.

amini

kubali au amini kwamba ni kweli

Romans 10:18

Lakini nasema, "Hawakusika?" Ndiyo, bila shaka

Paulo anatumia swali kwa msisitizo. "Lakini, nasema bila shaka Wayahudi wamesikia ujumbe kuhusiana na Kristo

Sauti yao imeenda katika inchi yote, na maneno yao mwisho mwa ulimwengu

Maelezo haya yote kwa msingi humaanisha kitu kile kile na yanatumiwa kwa msisitizo. Neno "yao" inarejea jua, mwezi, na nyota. Hapa wameelezwa kama wapeleka ujumbe kwa kuwaambia watu kuhusiana na Mungu. Hii inarejea kwa namna kuishi kwao uhushuhudia nguvu na utukufu wa Mungu. Inaweza kufanywa wazi kwamba Paulo ananukuu Maandiko hapa. "Kama ilivyoandikwa katika Maandiko, 'Jua, mwezi na nyota ni udhibitisho wa nguvu na utukufu wa Mungu, na kila aliye katika ulimwengu huyaona na ujua ukweli kuhusiana na Mungu"

Romans 10:19

Zaidi, nasema, "Waisraeli hawakujua"

Paulo anatumia swali kwa msisitizo. Neno "Israeli" urejea kwa watu walio ishi katika taifa la Israeli. "Tena nakwambia watu wa Israeli hawakujua ujumbe.

Kwanza Musa anasema, "Nitakukasirisha... Nitakuchochea

Hii ina maanisha kwamba Musa aliandika chini kile Mungu alisema. "Mimi" urejea kwa Mungu, na "wewe" urejea kwa Waisraeli. "Kwanza Musa anasema kwamba Mungu atakukasirisha...kukuchoea

kwa kipi siyo taifa

"kwa wale hautazamii kuwa ni taifa halisi" au "kwa watu wasio na taifa lolote"

Kwa maan ya taifa lisilo na uelewa

"kwa taifa lenye watu wale wasionijua mimi au amri zangu"

Nitakuchochea wewe kwa hasira

"Nitakufanya wewe kukasirika"

wewe

Hii inarejea kwa taifa la Israeli

Romans 10:20

Taarifa ya ujumla:

Hapa maneno "mimi" na "yangu" urejea kwa Mungu

Na Isaya ana ujasiri wa kutosha kusema

Hii ina maanisha nabii Isaya aliandika kile Mungu alikwisha sema.

Nilipatikana na wale ambao hawakunitafuta mimi

Pia, manabii mara nyingi huongelea mambo yajao kama vile yamekwisha tokea. Hii inasisitiza kwamba unabii bila shaka utatimia. "Ijapokuwa watu wa Mataifa hawatanitafuta, watanipata"

Nilionekana

"Nilifanya mwenyewe kuonekana"

anasema

"Yeye" ni Mungu, anaongea kupitia Isaya

Kwa siku yote

Kifungu cha maneno haya kinatumika kusisitiza mwendelezo wa juhudi za Mungu. "mwendelezo"

Nilinyosha mikono yangu watu wasio na utiifu na wabishi

"Nilijaribu kukukaribisha na kukusaidia, lakini ulikataa msaada wangu na kuendelea kutotii"

Romans 11

Warumi 11 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri huweka kila mstari wa mashairi upande wa kulia zaidi kuliko maandiko yote ili iwe rahisi kusoma. ULB hufanya hivi kwa mistari 9-10, 26-27, na 34-35, ambayo ni maneno kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

Kupandikiza

Paulo anatumia mfano ya "kupandikiza" kutaja mahali pa Wayunani na Wayahudi katika mipango ya Mungu. Kufanya mmea mmoja kuwa sehemu ya kudumu ya mmea mwingine inaitwa "kupandikiza." Paulo anatumia taswira ya Mungu kupandikiza Wayunani kama tawi la mwitu katika mipango yake ya kuokoa. Lakini Mungu hajawasahau juu ya Wayahudi, ambao wanasemwa kuwa mmea wa asili. Mungu atawaokoa pia Wayahudi wanaomwamini Yesu.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Je, Mungu alikataa watu wake? Hata kidogo"

Ikiwa Waisraeli (wazao wa kimwili wa Abrahamu, Isaka na Yakobo) wako katika mipango ya Mungu ya baadaye, au ikiwa wamebadilishwa katika mipango ya Mungu na kanisa, ni suala kuu la kitheolojia katika Sura ya 9-11. Maneno haya ni ya muhimu katika sehemu hii ya Warumi. Inaonekana kuonyesha kwamba Israeli bado hutofautiana na kanisa. Si wasomi wote wanafikia hitimisho hili. Licha ya kwamba wao wanakataa Yesu sasa kama Masihi wao, Israeli haijapungukiwa na neema na huruma ya Mungu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#christ and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#grace and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#mercy)

<< | >>

Romans 11:1

Maelezo yanayounganisha:

Japokuawa Israeli kama taifa lilikataliwa na Mungu, Mungu alitaka waelewe kuwa wokovu unakuja kwa neema bila kazi.

Basi naseema

"Mimi, Paulo, nikasema"

Je Mungu amewakataa watu wake?

Paulo alijiuliza hili swali ili awajibu maswali ya Wayahudi wengine waliokuwa wamekasirika kwamba Mataifa wamewekwa kuwa watu wa Mungu, wakati mioyo ya Wayahudi ikiwa imefanywa kuwa migumu.

Hata kidogo

"Hiyo haiwezekani" au "la hasha!" Ufafanuzi huu unakataa kwa nguvu kwamba hii haiwezi kutokea. Unaweza kuwa na ufafanuzi mwingine kwa lugha yako ambayo unaweza kutumia hapa.

Kabila la Benjamini

Hii inaelezea kabila ambalo ni kizazi cha Benjamini, moja kati ya makabila 12 ambayo Mungu aliwagawanya wana wa Israeli kwayo.

Aliowatambua

"Aliowafahamu tangu mwanzo"

Je, hamjui andiko linasema nini kuhusu Eliya, jinsi alivyomsihi Mungu juu ya Israeli?

"Hakika mnajua nini kimeandikwa kwenye maandiko. Mnakumbuka Eliya alivyomsihi Mungu juu ya Israeli."

Andiko linasema nini

Paulo anaelezea ni nini kimeandikwa kwenye maandiko.

Wao wamewauwa

"Wao" ni watu wa Israeli.

Nami nimesalia peke yangu

Neno "mimi" linamaanisha Eliya

Romans 11:4

Lakini ni nini Mungu alijibu akiwaambia?

Paulo anatumia swali hili kuwaleta wasomaji kwenye wazo linalofuata.

Ni nini jibu la Mungu akiwaambia

"Mungu aliwajibu vipi"

Yeye

Neno "yeye" linamaanisha Eliya

Watu elfu saba

"watu 7000"

Mabaki

Hapa inamaanisha sehemu ndogo ya watu waliochaguliwa na Mungu kupokea neema yake.

Romans 11:6

Lakini ikiwa ni kwa neema

Paulo anaendelea kuelezea namna neema ya Mungu inavyofanya kazi. "kwa kuwa neema ya Mungu inafanya kazi kwa rehema"

Ni nini basi?

"Tuhitimishe vipi?" "hivi ndivyo ambavyo tunapaswa kukumbuka."

Mungu amewapa roho ya ubutu, macho ili wasione, na masikio ili wasisikie

Huu ni ufafanuzi kuhusu ukweli kwamba niwabutu kiroho. Hawana uwezo wa kuona na kusikia ukweli wa kiroho.

Roho ya

Hapa inamaanisha "kuwa na tabia za" mfano "roho ya hekima."

Macho ili wasione

Kuona kwa jicho moja ilichukuliwa kuwa sawa na kupata uelewa.

Masikio ili wasisikie

Kusikia kwa masikio ilichukuliwa kuwa sawa na utii.

Romans 11:9

Acha meza zao ziwe na wavu

"Meza" inawakilisha sherehe, na "neti" au "mtego" inawakilisha adhabu. Nakusihi Mungu wakamate na uwatege katika sherehe zao"

Makwazo

"kitu kinachowafanya watende dhambi"

na kulipiza kisasi dhidi yao

"kitu kinachokuruhusu kulipa kisasi kwao"

Ukawainamishe migongo yao daima

Daudi alimuomba Mungu awafanye adui zake kuwa watumwa wanaobeba mizigo mizito kwenye migongo yao daima.

Romans 11:11

Maelezo yanayounganisha

Pamoja na kuwa Israeli kama taifa lililokataliwa na Mungu, Paulo anawaonya Mataifa kuwa makini na wasifanye kosa lile lile.

Wameona mashaka hata kuanguka?

"Je Mungu amewakataa daima kwa sababu wametenda dhambi?"

Hata kidogo

"Hiyo haiwezekani" au "la hasha!" Ufafanuzi huu unakataa kwa nguvu kwamba hii haiwezi kutokea. Unaweza kuwa na ufafanuzi mwingine kwa lugha yako ambayo unaweza kutumia hapa.

Dunia

Hapa inamaanisha watu wa duniani.

Romans 11:13

kuwatia wivu

Tafsiri kifungu hiki njia sawa kama alivyofanya katika (Rom:10:19)

walio mwili mmoja na mimi

Hii inamaanisha "Wayahudi wenzangu"

Romans 11:15

Kwao

Hii inawaelezea Wayahudi wasioamini

Dunia

Hii inamaanisha watu wa duniani.

kupokelewa kwao kutakuwaje ila uhai toka kwa wafu?

"Hivyo basi, Mungu atawapokea vipi wakimwamini Kristo? Itakuwa kama wamekuja tena kwenye uhai toka kwenye kifo"

Kama matunda ya kwanza ni takatifu, hivyo ni bonge la unga.

Paulo anamfananisha Ibrahimu, Isaka na Yakobo, mababu wa Israeli na ngano ya kwanza kuvunwa, na Waisraeli ambao ni uzao wa wanaume hao ni unga unaotokana na ngano itakayovunwa baadae.

Kama mizizi ni takatifu, vivyo hivyo na matawi

Paulo anamfananisha Ibrahimu, Isaka na Yakobo, mababu wa Israeli na mizizi ya mti, na Waisraeli ambao ni uzao wa wanaume hao kama matawi ya miti.

Takatifu

Mazao ya kwanza kuvunwa daima yanakuwaga "matakatifu" hii ni, yameachwa kwa ajili ya Mungu. Hapa "mazao ya kwanza" yanasimama kwa watu wa kwanza kumuamini Kristo.

Romans 11:17

Kama wewe, tawi pori la mizeituni

Neno "wewe" na "tawi pori la mizeituni" linaelezea Watu wa Mataifa walikubali wokovu kupitia Yesu.

Ulipandikizwa kati yao

"Walipachikwa kwenye mti kati ya matawi yaliyobaki"

Mizizi ya utajiri wa mizeituni

Hii inamaanisha ahadi za Mungu.

Usijisifu juu ya matawi

"Usisieme kuwa wewe ni bora zaidi ya Wayahudi waliokataliwa na Mungu"

si wewe ambaye unasaidia mizizi, bali mizizi inakusaidia wewe

Waamini wa Mataifa waliamini kuwa walikombolewa tuu kwa sababu ya agano la ahadi la Mungu lililofanywa kwa Wayahudi

Romans 11:19

Matawi yalikatwa

"Mungu aliyakata matawi"

Matawi

Neno hili limetumika kuwaelezea Wayahudi walikataliwa na Mungu.

Naweza kupandikizwa

maneno haya yametumika kuwaelezea waamini wa Mataifa waliokubaliwa na Mungu. "anaweza kunipachika"

"walikatwa"

"aliwakata"

wao... wale

Maneno "wao" au "wale" inamaanisha Wayahudi ambao hawakuamini.

Lakini wewe simama kwa imani yako

"Lakini ubaki kwa sababu ya imani yako"

Kwa maana ikiwa Mungu hakuyaachia matawi ya asili, je, unadhani atakuhurumia wewe

"Kwa maana ikiwa Mungu hakuyahurumia matawi ya asili, je, unadhani atakuhurumia wewe"

Matawi ya asili

Hii inamaanisha Wayahudi

Romans 11:22

matendo mema na ukali wa Mungu

Paulo anawakumbusha waamini wa Mataifa kwamba japokuwa Mungu amekuwa mwema sana kwao, hatasita kuwahukumu na kuwaadhibu.

Vinginevyo wewe pia utakatiliwa mbali

"Vinginevyo Mungu atakukatilia mbali"

Romans 11:23

kama hawataendelea katika kutoamini kwao

"Kama Wayahudi wanaanza kumiamini Kristo"

Watapandikizwa tena

"Mungu atawapandikiza tena"

Kupandikiza

Hii ni hatua ya kawaida ambapo tawi lililo hai la mti mmoja linapachikwa kwenye mti mwingine ili liweze kukua kwenye ule mti mpya.

Kwa maana ikiwa wewe ulikatwa nje kwa asili ya mzeituni mwitu, na kinyume cha asili walipandikizwa katika mzeituni ulio mwema, si zaidi sana hawa Wayahudi, ambao ni kama matawi ya asili kuweza kupandikizwa tena ndani ya mzeituni wao wenyewe?

"Ikiwa Mungu atakukata nje kwa asili ya mzeituni mwitu, na kinyume cha asili walipandikizwa katika mzeituni mzuri, si zaidi sana hawa Wayahudi, ambao ni matawi ya asili, kwenye mzeituni wao wenyewe?"

Matawi

Paulo anawafananisha wanachama wa watu wa Mungu na matawi ya mti.

Wao..... Wale

Ilipojitokeza "wao" au "wale" inamaanisha Wayahudi.

Romans 11:25

Sitaki ninyi msijue

"Natamani sana mtambue"

Mimi

Neno "mimi" linamaanisha paulo.

wewe...wewe... ninyi

Maneno haya "wewe" na "ninyi" yanamaanisha Mataifa walioamini.

ili kwamba msiwe na hekima katika kufikiri kwenu wenyewe.

Waamini wa mataifa wanaweza kuamini kwamba wana hekima zaidi kuliko Wayahudi wasioamini. "Ili msifikiri kwamba mna hekima zaidi ya mlivyo"

ubaguzi mgumu umetokea katika Israeli

Baadhi ya Wayahudi walikataa kukubali wokovu kupitia kwa Yesu.

hadi kukamilika kwa mataifa kutakapokuja

Neno "mpaka" linaelezea kuwa Wayahudi wengi wataamini baada ya Mungu kumaliza kuwaleta Mataifa kanisani.

Romans 11:26

Maelezo yanayounganisha

Paulo anasema mkombozi atakuja toka Israeli kwa utukufu wa Mungu.

Hivyo Israeli wote wataokoka

"Hivyo Mungu atawaokoa Waisraeli wote"

Waisraeli wote wataokoka

Hii imeongezwa chunvi. Wayahudi wengi wataokolewa.

Romans 11:28

Kwa upande mmoja... kwa upande mwingine

Hizi ni sentensi zinazotumika kufananisha vitu viwili tofauti kuhusu kitu. Paulo alitumia kuelezea kwamba Mungu aliwakataa Wayahudi, lakini pia bado anawapenda.

Wanachukiwa kwa sababu yenu

Upendo wa Mungu kwa Mataifa ulikuwa mkubwa sana kiasi kwamba ukilinganisha upendo kwa Wayahudi ukaonekana kama chuki.

Kwa kuwa walichukiwa

"Mungu aliwachukia Wayahudi"

Kwa ajili ya zawadi na wito wa Mungu usiobadilika

"Kwa sababu zawadi ya Mungu na wito wake hauwezi kubadilika"

Romans 11:30

Mlikuwa mmemuasi

"Hamkumtii hapo zamani"

Ninyi

Hii inamaanisha waamini wa Mataifa, na ni wingi.

Mungu amewafunga watu wote katika uasi

Hii pia inaweza kumaanisha Mungu anawafanya wasiweze kuacha kumuasi, kama wafungwa walioshindwa kutoroka gerezani. "Mungu amamfanya kila mtu kuwa mfungwa kwa kuasi"

Romans 11:33

Jinsi zilivyo kuu utajiri na hekima na maarifa ya Mungu!

"Jinsi zinavyoshangaza faida za hekima ya Mungu na maarifa"

Hazichunguziki hukumu zake, na njia zake ni zaidi ya kugundua

Hatuwezi kabisa kuelewa mambo ambayo anayaamua na kujua njia anazotumia juu yetu.

Romans 11:35

Hivyo atalipwa tena

"Hivyo Mungu atamlipa tena"

Kumlipa yeye

Neno "yeye" linamaanisha mtu aliyempa Mungu

yeye

Sehemu nyingine "neno" yeye linamaanisha MUngu

Romans 12

Warumi 12 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri huweka kila mstari wa mashairi upande wa kulia zaidi kuliko maandiko yote ili iwe rahisi kusoma. ULB inafanya hivyo kwa maneno ya mstari wa 20, ambayo yanayotoka Agano la Kale.

Wasomi wengi wanaamini kwamba Paulo anatumia neno "kwa hiyo" katika Warumi 12:1 kurejea kwenye Sura zote za 1-11. Baada ya kuelezea kwa uangalifu injili ya Kikristo, Paulo sasa anaelezea jinsi Wakristo wanapaswa kuishi kulingana na ukweli huu mkubwa. Sura ya 12-16 inazingatia kuishi kwa imani ya Mkristo. Paulo anatumia amri nyingi tofauti katika sura hizi kutoa maelekezo haya ya vitendo. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith)

Dhana maalum katika sura hii

Kuishi Kikristo

Chini ya sheria ya Musa, watu walitakiwa kutoa dhabihu za hekalu za wanyama au nafaka. Sasa Wakristo wanatakiwa kuishi maisha yao kama aina ya dhabihu kwa Mungu. Dhabihu za kimwili hazihitajiki tena. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lawofmoses)

Mifano muhimu ya matamshi katika sura hii

Mwili wa Kristo

Mwili wa Kristo ni sitiari muhimu au mfano inayotumiwa katika Maandiko kutaja kanisa. Kila mshiriki wa kanisa anafanya kazi ya kipekee na muhimu. Wakristo wanahitaji kila mmoja ya wenzao. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#body and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

<< | >>

Romans 12:1

Maelezo yanayounganisha:

Paulo anatuambia namna ambavyo maisha ya mwamini yanatakiwa yawe na namna waamini wanavyotakiwa kutumika.

Nawasihi Basi, ndugu, kwa huruma zake Mungu

"Waamini wenzangu, kwa sababu ya neemakuu ambayo Mungu ametupa nawasihi sana"

itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai

Hapa Paulo ametumia neno "miili" akimaanisha mtu. Paulo anamfananisha mwamini wa Kristo anayemtii Mungu na wanyama ambao Wayahudi waliwaua na kutoa sadaka kwa Mungu. "Mjitoe kabisa kwa Mungu mkiwa hai kama sadaka iliyokufa kwenye madhabahu hekaluni"

Takatifu, iliyokubalika na Mungu

Maana nyingine yaweza kuwa 1) "sadaka ambayo unampa Mungu pekee na itakayomtukuza" au 2) "Inayokubalika na Mungu kwa kuwa ni safi"

Hii ni huduma yenu ya kiroho

Inaweza kumaanisha 1) "Hii ni njia sahihi ya kumwabudu Mungu" au 2) "hii ndo namna ya kumwabudu Mungu kwenye roho zenu"

msiifuatishe namna ya dunia hii

Inamaanisha kwamba 1) "Msiishi kama dunia inavyoishi" au 2) Msifikirie kama dunia inavyofikiri."

Msiifuatishe

Hii inaweza kumaanisha 1) " Msiache dunia kuwaambia ni nini cha kufanya" au Msiache... nini cha kufikiria" au 2) "Msiruhusu kufanya kama dunia wanavyofanya"

Dunia hii

Hii inamaanisha watu wasioamini, wanaoishi katika dunia hii.

bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu.

"lakini muacheni Mungu awabadilishe namna mnavyofikiri" au "lakini mwacheni Mungu awabadilishe namna mnavyoenenda kwa kuwabadilisha kwanza namna mnavyofikiri"

Romans 12:3

kwa sababu ya neema niliyopewa,

Hapa "neema" inaelezea Mungu alivyomchagua Pulo kuwa Mtume na kiongozi wa kanisa. "Kwa kuwa Mungu alinichagua kuwa Mtume"

Kwamba kila mtu ambaye yupo miongoni mwenu hapaswi kufikiri zaidi juu yenu wenyewe kuliko mnavyopaswa kufikiri

"Kwamba mtu asifikiri kwamba ni bora zaidi ya watu wengine"

Badala yake, mnapaswa kufikiri kwa njia ya hekima

"Lakini mnapaswa kuwa na hekimakwa namna mnavyofikiri kuhusu ninyi wenyewe"

kama ambavyo Mungu amewapa kila mmoja kiasi fulani cha imani.

Ikiwa Mungu amewapa kila mmoja kiasi tofauti cha imani kwamba mnapaswa kufikiri kwa makini"

Romans 12:4

Kwa kuwa

Paulo anaelezea kwa nini Wakristo hawapaswi kufikiria kuwa wao ni wa maana zaidi ya wengine.

Tuna viungo vingi katika mwili mmoja

Paulo anawafananisha Waamini wote katika Krosto kama sehemu tofauti zamwili. Amefanya hivi kuonyesha japokuwa waamini wanamtumikia Kristo kwa njia tofauti, kila mtu ni mali ya Kristo na anamtumikia kwa njia ya muhimu.

Kiungo

Hivi ni vitu kama macho, tumbo, na mikono.

Mmoja mmoja kwa kila mmoja

"Kila mwamini ni sehemu ya mwili wa mwamini mwingine" "na kila muumini ameunganishwa pamoja na waamini wengine"

Romans 12:6

Tuna zawadi mbalimbali kufuatana na neema tuliyopewa

"Mungu ammempa kila mmoja wetu uwezo wa kufanya vitu tofauti kwa ajili yake"

Itendeke kwa kadiri ya imani yake

Inaweza kuwa na maana kuwa 1) "atoe unabii ambao hautazidi kiwango cha imani amabyo Mungu ametupa" au 2) "Aseme unabii unaokubaliana na mafundisho ya imani yetu."

Kama zawadi ya mtu ni kutoa

Maana inaweza kuwekwa wazi. "Ikiwa matu ana zawadi ya kutoa pesa au kitu chochote kwa wahitaji"

Romans 12:9

Pendo lisiwe na unafiki

"Acha upendo uwe wa wazi" au "Acha upendo uwe wa kweli"

Upendo

Hili ni neno lingine linalomaanisha upendo wa ndugu au upendo kwa rafiki au kwa wanafamilia. huu ni upendo wa asili wa binadamukati ya marafiki au ndugu.

Kuhusu upendo wa ndugu, mpendane

Paulo ameanza kuonyesha idadi ya vitu tisa, kila kimoja kikionyesha "Kuhusu....." "kuwaambia waamini wanapaswa kuwa watu wa aina gani.

Kuhusu upendo wa ndugu

"Kwa namna ambavyo unaweza kumpenda mwamini mwenzako"

Mpendane

"Muwe na uaminifu" kama wanafamilia.

Kuhusu heshima, mheshimiane.

"Waheshimu na watii wengine" au, tumia sentensi mpya, "Kama unavyowaheshimu waamuni wenzako, watii"

Romans 12:11

Kuhusu bidii, msiwe na wasiwasi. Kuhusu roho, myatamani. Yanayohusu Bwana, mtumikieni.

"Msiwe wavivu kwenye zamu zenu, bali mtamani kumfuata roho na kumtumikia Bwana"

Furahini kwa ujasiri mlionao kuhusu siku zijazo.

"Kuweni na furaha maana ujasiri wenu upo katika Mungu"

Mvumilie katika matatizo yenu

"Muwe wavumilivu wakati mgumu unapokuja"

Endeleeni kuomba

"Na mkumbuke kuomba kila mara"

Mshiriki katika mahitaji ya waumini.

Hili ni jambo la mwisho kwenye orodha inayoanza "Kuhusu mahitaji ya waamini, mshiriki pamoja nao" au "Ikiwa" au "Wakristo wenzako wakiwa na tatizo, musaidie kile wanachohitaji"

Mtafute njia nyingi za kuonesha ukarimu.

"Muwakaribishe nyumbani kwenu ikiwa wanahitaji mahali pa kukaa"

Romans 12:14

Muwe na nia moja ninyi kwa ninyi

"Mkubaliane ninyi kwa ninyi" au "muishi kwa umoja ninyi kwa ninyi"

Msifikiri kwa njia ya kujivuna

"Msifikiri kuwa ninyi ni bora sana kuliko wengine"

Muwakubali watu wa hali ya chini

"Wakaribisheni watu mnaoona hawana umuhimu"

Msiwe na hekima juu ya mawazo yenu wenyewe

"Msifikiri kuwa ninyi mna hekima nyingi kuliko mtu yeyote yule"

Romans 12:17

Msilipe ovu kwa ovu

"Msifanye yaliyo maovu kwa mtu aliyewafanyia maovu"

Fanyeni mambo mema machoni pa watu wote

"Fanyeni mambo ambayo kila mtu ataona ni mazuri"

Kama ilivyowekwa kwenu, kuweni na amani na watu wote

"Fanyeni lolote mnaloweza kuwa na amani na kila mtu"

Kama ilivyowekwa kwenu

"Kama mnavyoweza kudhibit na ni wajibu kwa"

Romans 12:19

Kisasi ni changu; nitalipa

Mistari hii miwili inamaanisha kitu kimoja kwa kusisitiza kwamba Mungu atawalipiza watu wale. "Nitawalipiza ninyi"

Adui yako .... mlishe..... mnyweshe... ukifanya hivi, utakusanya ... Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya

Aina zote za "wewe" au "yako" inamuelezea mtu mmoja.

Lakini adui yako akiwa na njaa.... kichwa chake

Paulo ananukuu sehemu nyingine ya maandiko. "Lakini pia imeandikwa, 'ikiwa adui yako ana njaa... kichwa chake"'

Mlishe

"Mpe chakula"

Kusanya makaa ya moto juu ya kichwa chake

Paulo anafananisha adhabu watakayoipata maadui na kaa la moto linalowekwa kwenye vichwa vyao. maana nyingine zaweza kuwa 1)"kumfanya mtu aliyekuumiza kujisikia vibaya kwa namna alivyokutendea" au 2) "Kumpa Mungu sababu ya kuwahukumu adui zako vibaya zaidi"

Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya kwa wema

Paulo anauelezea "ubaya" kama kitu kinachoishi. "Msiwaache waliowaovu wawashinde, ila muwashinde kwa kufanya yaliyo mema."

Romans 13

Warumi 13 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Katika sehemu ya kwanza ya sura hii, Paulo anawafundisha Wakristo kutii viongozi wao. Wakati huo, watawala wa Kirumi wasiomcha Mungu walitawala nchi hiyo. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#godly)

Dhana maalum katika sura hii

Watawala wasiomcha Mungu

Wakati Paulo anafundisha juu ya kuitii watawala, wasomaji wengine wataona kuwa vigumu kuelewa, hasa katika maeneo ambapo watawala wanatesa kanisa. Wakristo lazima watii wakuu wao pamoja na kumtii Mungu, isipokuwa wakati watawala hawaruhusu Wakristo kufanya kitu ambacho Mungu anawaagiza. Kuna wakati ambapo mwamini lazima awe chini ya watawala hawa na kuteseka kwa mikono yao. Wakristo wanaelewa kwamba ulimwengu huu ni wa muda mfupi na watakuwa na Mungu milele. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#eternity)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Mwili

Hili ni suala gumu. Kuna uwezekano kuwa "Mwili" ni mfano ya asili yetu ya dhambi. Paulo hafundishi kwamba miili yetu ya kimwili ni dhambi. Inaonekana kuwa Paulo anafundisha kwamba wakati wote Wakristo wanaishi ("katika mwili"), tutaendelea kutenda dhambi. Lakini asili yetu mpya itapigana dhidi ya asili yetu ya zamani. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#flesh and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

<< | >>

Romans 13:1

Sentensi unganishi

Paulo anawaambia waamini jinsi ya kuishi chini ya watawala wao.

Na kila nafsi iwe tiifu

"Kila mkristo anapaswa kutii"

Mamlaka iliyo juu

"Watawala wa srikali."

Kwa ajili ya

"Kwa sababu"

Hakuna mamlaka isipokuwa inatoka kwa Mungu

"Mamlaka yote yatoka kwa Mungu"

Mamlaka iliyopo imewekwa na Mungu

"Watu walio katika mamlaka wapo kwa sababu Mungu amewaweka pale"

Mamlaka hiyo

"Hiyo mamlaka ya kiserikali"

Wale waipingao

" Wale wanaopinga mamlaka ya kiserikali"

Romans 13:3

Kwa kuwa

Paulo anaeleza nini kitatokea ikiwa serikali itamtia hatiani mtu.

Watawala si watu wa kuogofya

Watawala hawafanyi watu waogope.

Kwa mema... kwa maovu

Watu hutambulika kwa " matendo yao mema" au " matendo yao mabaya"

Je unatamani kuwa mwenye kuogopa mamlaka

"Ngoja nikueleze jinsi ya kuogopa mamlaka"

Utasifiwa kutokana na hiyo

Serikali itasema mambo mazuri juu ya wale watendao mema.

Habebi upanga bila sababu

"Anabeba upanga kwa sababu iliyo njema" au " anauwezo wa kuwaadhibu watu, na atawaadhibu watu."

Mlipakisasi kwa gadhabu

" Mtu anaye adhibu watu kama maelezo ya hasira ya serokali dhidi ya maasi"

Si tu kwa sababu ya gadhabu, lakini pia kwa sababu ya dhamiri.

"Siyo tu kwamba serikali haitawaadhibu, bali pia utakuwa na dhamiri safi mbele za Mungu"

Romans 13:6

Kwa sababuya hili

"Kwa sababu serikali huwaadhibu watenda maovu"

Wewe ... lipa kwa kila mtu

Paulo hapa anawambia waamini.

Kwa

" Hii ni sababu kwa nini unapaswa kulipa kodi"

Hudumia

"Toa huduma" au "fanya kazi"

Ushuru

Hii inamaanisha fedha unayolipa kw aajili ya ushuru.

Romans 13:8

Senensi unganishi

Paulo anawaambia waamini jinsi ya kufanya kwa majirani.

Usidaiwe na mtu kitu chochote

"Lipa unachodaiwa na serikali na kila mtu yeyote"

Usidaiwe

Tendo hili liko katika hali ya u wingi na linawahusu waamini wote wa Rumi.

Upendo

Hii ina maanisha upendo ambao unatoka kwa Mungu ambao unaelekeza mazuri kwa wengine, hata kama haimfaidii mtu mwenyewe.

Isipokuwa

Sentensi mpya: " Kuwapenda wakristo wengine ni deni moja ambalo unaweza kuendelea kudaiwa"

Uta

Mahali popote palipo na neno "uta" katika 13:9 ni katika hali ya umoja, ingawa mwandishi alikuwa akiwaambia kundi la watu kana kwamba alikuwa mtu mmoja, kwa hiyo unaweza kutumia neno lenye kuonesha u wingi hapa.

Tamani

Kutamani kuwa au kumiliki kitu fulani ambacho mtu hana na asingeweza kuwa nacho au kumiliki.

Upendo haudhuru

Sentensi hii inaonesha upendo kama mtu aliye mwema kwa watu wengine. " Watu wanao penda wenzao hawawezi kuwadhuru."

Kwahiyo

"Kwa sababu upendo haudhuru jirani wa mtu"

Romans 13:11

Usiku umeendelea sana

" Wakati uliopo wa dhambi umekaribia kumalizika"

Siku imekaribia

"Kristo atarudi upesi"

Matendo ya giza

Haya ni matendo maovu ambayo watu wanpendelea kuyafanya usiku, wakati hakuna mtu anaye weza kuwaona.

Tuvae silaha za nuru

" Inatupasa kumruhusu Mungu kutulinda kwa kufanya tu yale ambayo tunataka watu waone tunayafanya"

Romans 13:13

Nasi tu...

Paulo anajumlisha wasomaji wake na waamini wengine pamoja na yeye mwenyewe.

Kama katika siku

"Katika hali ya kuonekana" au tukijua kuwa kila mtu anaweza kutuona"

Ugomvi

Hii inamaanisha njama dhidi ya na mabishano na watu wengine.

Wivu

Hii inamaanisha hisia hasi ya mtu dhidi ya mafanikio ya mtu mwingine au faida juu ya mtu mwingine

Mvae Bwana Yesu Kristo

Hii inamaanisha kukubali asili mema ya Kristo kana kwamba ni vazi letu la juu ambalo watu wanaweza kuona.

Vaa

Kama lugha yako ina usemi wa wingi wa maagizo, unaweza kutumia hapa.

Usitoe mwanya kwa mwili

"Usiupe nafasi yoyote moyo wako wa zamani kufanya mambo mabaya"

Mwili

Hapa inamaanisha asili ya dhambi ya mtu.

Romans 14

Warumi 14 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri huweka kila mstari wa mashairi upande wa kulia zaidi kuliko maandiko yote ili iwe rahisi kusoma. ULB inafanya hivi kwa mstari wa 11 wa sura hii, ambayo Paulo ananukuu kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

Dhaifu katika imani

Paulo anafundisha kwamba Wakristo wanaweza kuwa na imani ya kweli na wakati huo huo kuwa "dhaifu katika imani" katika hali fulani. Hii inaelezea Wakristo ambao imani yao ni changa, haina nguvu, au haijaeleweka.(See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith)

Vikwazo vya chakula

Dini nyingi katika inchi ya kale ya Mashiriki ya Karibu zilizuia kile kilicholiwa. Wakristo wana uhuru wa kula kile wanachotaka. Lakini wanahitaji kutumia uhuru huu kwa hekima, kwa namna ambayo huheshimu Bwana na haisababishi wengine kutenda dhambi. ((See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin))

Kiti cha hukumu cha Mungu

Kiti cha hukumu cha Mungu au Kristo kinamaanisha wakati ambapo watu wote, ikiwa ni pamoja na Wakristo, watahukumiwa kwa jinsi walivyoishi maisha yao.

<< | >>

Romans 14:1

Sentensi unganishi

Paulo anawatia moyo waamini kukumbuka kuwa wana wajibika kwa mungu.

Wadhaifu katika imani

Hii inamaanisha wale ambao waliona hatia juu ya kula na kunywa vitu kadha wa kadha.

Bila kutoa hukumu kwa maswali hayo

"Na msiwalaumu kutokana na maoni yao"

Kwa upande mmoja, mtu mmoja anaimani kula chochote, bali kwa upande mwingine

Sentensi "Kwa upande mmoja" na "kwa upande mwingine" inatambulisha njia mbili tofauti za kuwaza juu ya kitu fulani. " Mtu mmoja ana imani kula kitu chochote lakini"

Romans 14:3

Wewe ni nani, wewe unaye hukumu mtumishi ambaye ni mali ya mtu mwingine?

Paulo anatumia swali kukemea wale wanao hukumu wengine. " wewe si Mungu, na hunaruhusa ya kuhukumu mojawapo wa watumishi wake"

Wewe, wewe

U-moja

Ni mbele ya bwana wake kuwa anasimama au kuanguka

"Ni bwana wake tu anaweza kuamua ikiwa atamkubali mtumishi au atamkataa"

Lakini atamfanya asimame, kwa kuwa Bwana ana uwezo wa kumsimamisha.

"Lakini Bwana atamkubali kwa sababu anauwezo wa kumfanya mtumishi akubalike"

Romans 14:5

Kwa upande mmoja, mtu huthamini siku moja kuliko nyingine. kwa upande mwingine, mtu huthamini sikuzote sawasawa.

Sentensi "kwa upande mmoja na kwa upande mwingine" vinatambulisha njia mbili za kufikiri juu ya kitu. " Mtu mmoja anafikiri siku moja ni ya muhimu kuliko zingine zote, lakini mtu mwingine anafikiri kwamba siku zote ni sawa"

Acha kila mtu ashawishike ndani ya fikra zake

Maana halisi inaweza kuelezwa. "ila mtu awe na uhaika wa kuwa anachofanya anamheshimu Mungu"

Yule ashikaye siku, anashika kwa ajili ya Bwana

"Mtu anaye abudu katika siku fulani hufanya kwa kumtii Bwana"

Na yule alaye, anakula kwa ajili ya Bwana

"Kila mtu anaye kula aina zote za chakula hufanya hivyo kwa ajili ya kumtii Bwana"

Yeye asiye kula, hujizuia kutokula kwa ajili ya Bwana

" Mtu asiye kula baadhi ya vyakula anafanya hivyo kwa ajili ya Bwana"

Romans 14:7

Sisi

Paulo anajumlisha wasomaji wake.

Wafu na wanaoishi

"Wale waliokufa na wale ambao wanaishi

Romans 14:10

Kwa nini unamuhukumu ndugu yako? Na wewe kwa nini unamdharau ndugu yako?

Paulo anaeleza jinsi ambavyo anaweza kuwakemea miongoni mwa wale wasomaji wake. "Ni vibaya kwako kumhukumu ndugu yako, na ni vibaya kwako kumdharau ndugu yako!" au " Usimuhukumu na kumdharau ndugu yako!"

Kwa sababu sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha Mungu

"Kiti cha hukumu"kinaashiria mamlaka ya Mungu ya kuhukumu. kwa kuwa Mungu atatuhukumu sisi sote"

Kama niishivyo

Sentensi hii inatumika kuanzisha kiapo au kiapo makini. "Unaweza kuwa na uhakika kuwa hii ni kweli"

Kwangu mimi kila goti litapigwa, na kila ulimi utatoa sifa kwa Mungu

Paulo anatumia maneno "Goti" na "ulimi" kumaanisha mtu. Pia,Bwana anatumia neno "Mungu" kumaanisha yeyemwenyewe. " Kila mtu atainama na kutoa sifa kwangu"

Romans 14:12

Atatoa hesabu yake kwa Mungu

"atatoa maelezo ya matendo yetu kwa Mungu

Lkini badala yake amua hivi, kwamba hakuna mtu atakaye weka kitu cha kujikwaa au mtego kwa ndugu yake

Hapa "kitu cha kujikwaa" na "mtego" inamaanisha kitu kilekile. " Lakini fanya kuwa lengo lako kutofanya au kusema neno lolote ambalo linaweza kumfanya mwamini mwenzako kufanya dhambi"

Ndugu

Hapa hii inamaanisha mwamini mwenzako, ikijumuisha wanawake na wanaume.

Romans 14:14

Najua na ninashawishika katika Bwana Yesu

Hapa maneno "jua" na " Ninashawishika" yanamaanisha kitu kilekile; Paulo anayatumia kusisitiza uhakika wake. "Nina uhakika kwa sababu ya mahusiano yangu na Bwana Yesu"

Hakuna kilicho safi kwa ajili yake chenyewe

"Kila kitu chenyewe ni safi"

Kwa ajili yake mwenyewe adhaniye kuwa ni safi, kwake yeye si safi

Lakini kama mtu akidhani kuwa kitu fulani si safi, hivyo kwake yeye si safi na anapaswa kuwa mbali nacho"

Ikiwa ni kwa sababu ya chakula ndugu yako anaumia

"Ikiwa utaumiza imani ya mwamini mwenzako kwa mabo ya chakula." hapa neno "yako" linamaanisha imani thabiti na " ndugu" linamaanisha aliye dhaifu katika imani.

Hautembei tena katika upendo

"Hauoneshi tena upendo"

Romans 14:16

Usifanye matendo yako mema yakasababisha watu kuwadhihaki

"Usifanye mambo, hatakama unadhani mambo hayo kuwa ni mazuri, ikiwa kama watu watasema ni mabaya"

Matendo yako mema

Hii inamaanisha matendo ya watu ambao ni imara katika imani.

Watu

Maana zaweza kuwa 1. waamini wengine, au 2. wasio amini.

Kwa kuwa ufalme wa Mungu siyo juu ya chakula na vinywaji, bali kwaajili ya haki, amani, na furaha katika Roho Mtakatifu

"Kwa kuwa Mungu hakuandaa ufalme wake ili aweze kutawala kile tunacho weza kula na kunywa. aliandaa ufalme wake ili kwamba tuweze kuwa na mahusiano na yeye na Roho Mtakatifu aweze kutupatia amani na furaha"

Romans 14:18

Amethibitishwa na watu

"Watu wata mthibitisha" au " watu watamuheshimu"

Tutafute mambo ya amani na mambo ambayo yatawajenga kila mtu na wenzake.

"Tutafute kuishi kwa amani na kusaidia mmoja na mwingine kukua katika imani"

Romans 14:20

Si jambo jema kula nyama, wala kunywa divai, wala chochote ambacho ndugu yako anaona ni vibaya

"Ni afadhali usile nyama au kunywa divai au chochote ambacho kinawaza kumsababisha mwenzako afanye dhambi"

Yako

Hii inamaanisha imani thabiti na "Ndugu" inamaanisha ndugu aliye dhaifu.

Romans 14:22

Hizi imani ambazo mlizo nazo

Hii inamaanisha imani juu ya vyakula na vinywaji

Wewe mwenyewe

U- moja kwa sababu Paulo anawambia waamini, unaweza kutumia tafsiri ya u-wingi.

wamebarikiwa wale jihukumu katika jambo ambalo anathibitika

"Wamebalikiwa watu ambao hawawezi kuhisi hatia kwa yale wanayo kusudia kufanya"

Ambaye anamashaka amehukumiwa ikiwa atakula

"Mungu atasema kwamba mtu hufanya vibaya ikiwa hana uhakika kama ni sawa kula chakula fulani, lakini hatahivyo anakula" au "Mtu ambaye hana uhakika kama ni sawa kula chakula fulani na anakula atakuwa na shida katika dhamiri"

Kwa sababu haitokani na imani

"Mungu atasema kuwa ni vibaya kwa sababu anakula kitu amabacho anaamini Mungu hataki ale"

Jambo lolote lisilotokana na imani ni dhambi

Unafanya dhambi ikiwa unafanya jambo ambalo huamini kuwa Mungu anataka ulifanye"

Romans 15

Warumi 15 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri huweka kila mstari wa mashairi upande wa kulia zaidi kuliko maandiko yote ili iwe rahisi kusoma. ULB inafanya hivi kwa mistari 9-11 na 21 ya sura hii, ambayo ni maneno kutoka Agano la Kale.

Baadhi ya tafsiri zinaweka nukuu za maneno ya kawaida kutoka Agano la Kale upande wa kulia zaidi kwenye ukurasa ili iwe rahisi kusoma. ULB inafanya hivyo kwa maneno yaliyotajwa katika mstari wa 12.

Katika Warumi 15:14, Paulo anaanza kuzungumza kibinafsi zaidi. Anabadilisha kutoka mafundisho na kuzungumzia mipango yake binafsi.

Mifano muhimu ya matamshi katika sura hii

Wenye nguvu/dhaifu

Maneno haya hutumiwa kurejea watu ambao wamekomaa na wachanga katika imani yao. Paulo anafundisha kwamba wale wenye nguvu katika imani wanastahili kuwasaidia walio dhaifu katika imani. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith)

<< | >>

Romans 15:1

Kauli unganishi

Paulo ana hitimisha hii sehemu kuhusu maisha ya muumini kwa ajili ya wengine kwa kuwakumbusha jinsi Kristo alivyoishi.

Sasa

Tafasri hili kwa kutumia maneno katika lugha yako linalotumika kutambulusha wazo jipya katika mdahalo.

sisi tulio na nguvu

"sisi tulio na nguvu katika imani

Sisi

Kkiwakilishi hiki cha jina kinamwelezea Paulo, wasomaji wake na waumini wengine

dhaifu

"wale ambao ni dhaifu katika imani"

kumwimarisha

Kuimarisha imani yake

Romans 15:3

Matusi ya wale waliokutukana yamenipata mimi

"Matusi ya wale waliomtukana Mungu yamempata Kristo pia"

Kwa chochote kilichotangulia kuandikwa, kiliandikwa kwa kutuelekeza

"Kila kitu kilichoandikwa katika maandiko wakati uliopita kiliandikwa kutujulisha sisi"

yetu...sisi

Paulo anawaunganisha wasomaji wake na waumini wengine.

Romans 15:5

Kauli Unganishi

Paulo anawatia moyo waumini kukumbuka kwamba wote waumini mataifa na wayahudi ambao wameamini wamefanywa mmoja katika Kristo.

na...Mungu...akupatie

"Omba kwamba...Mungu atakupa.

"kuwa na nia sawa kwa kila mmoja

"kuwa kwenye makubaliano na kila mmoja" au " kuwa na muunganiko"

Kumsifu kwa kinywa kimoja

"kusifu kwa pamoja kama vile ni kinywa kimoja kilikuwa kinaongea"

Romans 15:8

Kwakuwa nasema

Neno "Mimi linafafanua juu ya Paulo.

"Kristo amefanywa mtumishi wa tohara

Yesu Kristo alikuja kuwasaidia Wayahudi"

ili kwamba aweze kuthibitisha ahadi walizopewa mababa

"kwamba Mungu aweze kuzithibitisha ahadi alizowapa mababa wa Wayahudi"

kama ilivyoandikwa

"kama ilivyoandikwa kwenye maandiko"

na kwa mataifa

"na Kristo amefanywa mtumishi wa mataifa"

Romans 15:10

Tena inasema

"Tena andiko linasema" au Tena Musa anasema"

pamoja na watu wake

"pamoja na watu wa Mungu"

Kumsifu yeye

"Kumsifu Mungu"

Romans 15:12

shina la Yese

Yese alikuwa baba wa kimwili wa Mfalme Daudi. "uzao wa Yese"

Watu wa Mataifa watakuwa na ujasiri ndani yake

"Yeye/yake" hapa inamaanisha uzao wa Yese, ambaye ni Masihi.

Romans 15:13

Mungu wa tumaini

"Mungu, ndani yake tunatumaini"

awajaze na furaha yote na amani

"awajaze na furaha kuu na amani"

muweze kuzidi katika tumaini

"muweze kuwa na tumaini kamilifu"

Romans 15:14

Sentensi unganishi:

Paulo anawakumbusha waumini wa Rumi kwamba Mungu alimchagua ili kuwafikia mataifa kwa injili.

kujazwa na maarifa yote

"kujazwa na elimu ya kutosha katika kumfuata Mungu"

pia kuonyana kila mmoja na mwenzake

"pia kuweza kumfundisha kila mmoja"

Romans 15:15

kipawa nilichopewa na Mungu

Kipawa hiki ni kile alichochaguliwa kuwa mtume bila kujali mateso aliyowatendea waumini kipindi cha kuamini kwake. "kipawa ambacho Mungu alinipa"

kujitoa kwa mataifa uweze kukubaliwa

"Mungu anaweza kupendezwa na mataifa iwapo wanamtii yeye"

Romans 15:17

Hivyo furaha yangu iko katika Kristo Yesu na katika mambo ya Mungu.

"Kwahiyo nina sababu ya kufurahi katika Kristo Yesu na katika kazi ya Mungu aliyonipa kuitenda"

Haya mambo yametimizwa kwa neno na kwa tendo, kwa nguvu za ishara na maajabu, na kwa nguvu za Roho mtakatifu

"Kwa ajili ya utii wa mataifa, pekee nitanena kile Kristo ametimiza kupitia kwangu katika maneno na matendo yangu kwa nguvu za ishara na ajabu kupitia nguvu za Roho Mtakatifu."

ishara na maajabu

maneno haya mawili hakika yana maana moja ya miujiza ya namna tofauti tofauti.

ili kwamba kutoka Yerusalemu, na kuzungukia mbali kama Iliriko

Hii ni kutoka mji wa Yerusalemu na umbali kwenda jimbo la Iliriko, mkoa ulio karibu na Italia.

Romans 15:20

Kwa njia hii, tamaa yangu imekuwa kuitangaza injili, lakini si mahali Kristo anajulikana kwa jina

"Kwasababu hii, Ninataka huihubiri habari njema katika sehemu ambazo kamwe hazijasikia habari za Kristo"

Ambao kwa yeye hawana habari zake aliyekuja

"Wale ambao hakuna hata mmoja alishawaambia habari zake"

Romans 15:22

Sentensi unganishi:

Paulo anawaambia waumini wa Rumi kuhusu mipango yake ya kwenda Yerusalemu na anawaomba waumini kuombea.

Nilikuwa pia nimezuiliwa

Haina umuhimu kumtambua aliyekua amemzuia Paulo. "Walinizuia" au "watu walinizuia"

sina tena sehemu yoyote katika mikoa hii

Paulo anamaanisha kuwa hakuna sehemu katika maeneo haya wanamuishi watu ambapo Injili haijahubiriwa

Romans 15:24

katika kupita

"kama na kwenda kupitia Rumi" au "wakati niko safarini"

kufurahia ushirika wenu

"kufurahi kutumia kiasi cha muda pamoja nanyi" au "Kufurahi kuwatembelea"

Hispania

Hili ni jimbo magharibi mwa mji wa Rumi ambapo Paulo alitamani kupatembelea

Romans 15:26

Ndiyo, ilikuwa kwa upendo wao

"Waumini wa Makedonia na Akaya walipendezwa kutenda" au "walifurahia kutenda"

hakika wamekuwa wadeni wao

"hakika watu wa Makedonia na Akaya ni wadeni kwa waumini wa Yerusalemu"

ikiwa mataifa wameshiriki katika mambo yao ya kiroho, wanadaiwa na wao pia kuwahudumia

"tangu mataifa wameshiriki mambo ya rohoni na waumini wa Yerusalem, Mataifa wanadai huduma kwa waumini wa Yerusalemu"

Romans 15:28

utoshelevu

"Kutimizwa katika usalama"

tunda

Neno hili linazungumzia fedha.

Nitakuja katika utimilifu wa baraka za Kristo.

"Nitakuja na baraka kamilifu za Kristo"

Romans 15:30

Sasa

Kama lugha yako ina namna ya kuonyesha Paulo ameacha kuongelea kuhusu mambo mazuri ana tumaini. Na sasa anaanza kuzungumzia juu ya hatari anayokutana nayo, itumie hapa.

Ninawasihi

"Ninawatia moyo"

ndugu

"Hapa ina maana ya kujumuisha waumini wote wa kiume na wa kike.

shiriki

"tenda kwa bidii" au "hangaika"

kuokolewa

"Kuokolewa toka hatari" au "kulindwa"

Romans 15:33

na Mungu wa amani

"Mungu wa amani" inamaanisha Mungu anayewafanya walioamini wawe na amani thabiti.

Romans 16

Warumi 16 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Katika sura hii, Paulo anatoa salamu za kibinafsi kwa Wakristo wengine huko Roma. Ilikuwa kawaida kumaliza barua na aina hii ya salamu ya kibinafsi katika inchi za kale ya Mashariki ya Karibu.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Kwa sababu ya hali ya kibinafsi ya sura hii, mengi juu ya mazingira hayajulikani. Hii itafanya tafsiri iwe ngumu zaidi. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

__<< | __

Romans 16:1

Kauli unganishi

Kisha Paulo anasalimia waumini walio wengi huko Rumi kwa kutaja majina

Namkabidhi kwenu Fibi

"Nawaomba mumheshimu Fibi"

Fibi

Hili ni jina la mwanamke

dada yetu

Neno hili linamwelezea Paulo na waumin9 wote. "Dada yetu katika Kristo"

Kenkrea

Hii ilikuwa ni bandari ya mji wa Giriki.

Mpokee katika Bwana

"Mkaribisheni kwasababu sisi sote tumemilikiwa na Bwana"

Katika kicho cha thamani cha waumini

" katika njia ambayo waumini wangeweza kukaribisha waumini wengine"

simama pamoja naye

"Mmusaidie"

amekuwa mhudumu wa wengi na wangu mwenywe pia

"amewahudumia watu wengu, na amenisaidia mimi pia"

Romans 16:3

Prisila na Akila

Priska anajulikana kama Prisila, alikuwa mke wa Akila

watenda kazi nami katika Kristo Yesu

"Ambaye anatenda kazi na mimi kuwaambia watu habari za Yesu Kristo"

lisalimie kanisa lililo katika nyumba yao

"Wasalimie waumini ambao hukutana nyumbani mwa nyumba ya Mungu.

Epanieto

Hili ni jina la mwanaume

mzaliwa wa kwanza katika Asia kwa Kristo

kivumishi hiki kinamaanisha kuwa Epanieto alikuwa mtu wa kwanza katika Asia kumwamini Yesu.

Romans 16:6

Mariamu

Hili ni jina la Mwanamke.

Yunia

Hili linaweza kuwa 1) Yunia ni jima la mwanamke, au siyo vile, 2) Yunia ni jina la mwanaume.

Anroniko...Ampliato

Haya ni majina ya wanaume.

mpendwa wangu katika Bwana

"rafiki yangu mpendwa na muumini mwenzangu"

ni maarufu miongoni mwa mitume

Hii inaweza kutafasiriwa kama "Mitume wanawafahamu vyema"

Romans 16:9

Urbano...Stakisi...Apele...Aristobulo...Herodioni... waliokubaliwa katika Kristo

Haya ni majina wa wanaume.

kukubaliwa katika Kristo

neno "kukubaliwa" linamaanisha kwamba mtu amejaribiwa na kuthibitishwa kuwa mkweli.

walio katika Bwana

hii inamaanisha wale wote walioweka tumaini katika Yesu.

Romans 16:12

Turufena...Trifosa...Pesisi

Haya ni majina ya wanawake

Rufio...Asikrito...Flegoni...Heme...Patroba...Hema

Haya ni majina ya wanaume.

aliyechaguliwa katika Bwana

"ambaye Mungu amemchagua" kwasababu ya sifa maalumu.

mama yake na wangu

"mama yake, ambaye namfikiria kama mama yangu"

Romans 16:15

Filogo...Neria...Olipa

Haya ni majina ya wanaume.

Yulia

Jina la mwanamke ambaye pengine alikuwa ameolewa na Filologo.

busu takatifu

jinsi ya kuonesha hisia za upendo kwa wumini wenzako

Romans 16:17

Kauli unganishi

Paulo anatoa onyo la mwisho kwa waumini kuhusu umoja na kuishi kwa ajili ya Mungu

tafakari juu ya

"kuwa waangalifu kwa"

ambao wanasababisha mgawanyiko na vipingamizi

"ambao wanasababisha waumini kubishana kila mmoja kwa mwingine na kuacha kuwa na imani kwa Mungu"

Wanakwenda kinyume na mafundisho ambayo mmekwisha kujifunza

'Wanafundisha mafundisho ambayo hayakubaliani na ukweli mliokwisha jifunza tayari"

Geukeni mtoke kwao

"jitengeni mbali na wao"

bali kwa matumbo yao wenyewe

Hapa "tumbo" linafafanua tamaa za kimwili. "Lakini wanataka kufurahisha tamaa zao mbaya"

Kwa maneno yao laini na pongezi za uongo

Maneno "laini" na "pongezi za uongo" kimsingi yana maana moja. Paulo anafafanua jinzi gani hawa watu wanavyowadanganya waumini. "kwa kusema mambo ambayo yanaonyesha ni mema na ya kweli"

kutokuwa na hatia

"ambao hawana hatia wanawatumainia wao" au "ambao hawawajui hawa waalimu wanaowatia upumbavu"

Romans 16:19

Kwa mfano wa utii wenu mwamfikia kila mmoja

"Wakati mnapomtii Yesu kila mmoja husikia hivyo"

Mungu wa amani hatakawia kumwangamiza Shetani chini ya nyayo zenu

Kivumishi "kumwangamiza chini ya nyayo" kinafafanua ushindi kamili juu ya adui. "Mungu hatakawia kukupa amani ya ushindi kamili dhidi ya Shetani"

bila hatia mbele ya uovu

"Bila kuchanganywa katika uovu"

Romans 16:21

Kauli unganishi

Paulo anatoa salamu kutoka kwa waumini ambao wako pamoja naye.

Lukio...Yasoni...na Sospeter...Tertio

Haya ni majina ya wanaume.

Tertio

Tertio ndiye mwanaume aliyeandika yale Paulo aliyoyafundisha.

Nawasalimu katika Bwana

"Nawasalimu ndugu waumini katika Bwana"

Romans 16:23

Gayo...Erasto...Kato

Haya ni majina ya wanaume

mwenyeji

Inamaanisha waumini waliokutana katika nyumba yake na kuabudu.

mtunza hazina

Huyu mtu ndiye aliyekuwa akitunza fedha ya kikundi.

Romans 16:25

Kauli unganishi

Paulo anahitimisha kwa maombi ya baraka

sasa

Neno hili "sasa" linaonyesha kufikia mwisho wa barua.

kufanya msimame

"kufanya imani yenu kuimarika"

kulingana na injili na mafundisho ya Yesu Kristo"

Habari njema ambayo nimeihubiri kuhusu Yesu Kristo

kulingana na ufunuo wa siri iliyofichwa kwa muda mrefu

"Kwa kuwa Mungu ameifunua siri kwetu waumini ambayo alikuwa ameitunza muda mrefu"

Lakini sasa imekwisha funuliwa na kufanywa kujulikana na maandiko ya unabii kulingana na amri ya Mungu wa milele

"Lakini sasa Mungu wa milele ameifanya ijulikane kupitia maandiko"

kwa utii wa imani miongoni mwa mataifa yote

"ili kwamba mataifa yote yatamtii Mungu kwasababu ya imani yao kwake"

Romans 16:27

kwa Mungu pekee mwenye hekima...kuwe na utukufu milele. Amina

Hapa "kupitia Yesu Kristo" kunaeleza kile ambacho Yesu alifanya. Kumpa utukufu kunamaanisha kumpa Mungu sifa.

Utangulizi wa 1 Wakorintho

Sehemu ya 1: Utangulizi wa Ujumla

Maelezo ya Kitabu cha 1 Wakorintho

  1. Mgawanyiko katika kanisa (1:10-4:21)
  2. Dhambi na makosa (5:1-13)
  3. Wakristo kuwapeleka Wakristo wengine mahakamani (6:1-20)
  4. Ndoa na mambo yanayohusiana nayo (7:1-40)
  5. Uovu wa uhuru wa Kikristo; chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu, kukimbia ibada ya sanamu; kufunika kwa vichwa vya wanawake (8:1-13; 10:1-11:16)
  6. Haki za Paulo kama mtume (9:1-27)
  7. Meza ya Bwana (11:17-34)
  8. Vipaji vya Roho Mtakatifu (12:1-31)
  9. pendo (13:1-13)
  10. Vipaji vya Roho Mtakatifu: unabii na lugha (14:1-40)
  11. Ufufuo wa waumini na ufufuo wa Kristo (15:1-58)
  12. Kufunga: mchango wa Wakristo huko Yerusalemu, maombi, na salamu za kibinafsi (16:1-24)

Nani aliandika Kitabu cha 1 Wakorintho?

Paulo aliandika 1 Wakorintho. Paulo alitoka mji wa Tarso. Alikuwa anajulikana kama Sauli katika maisha yake ya awali. Kabla ya kuwa Mkristo, Paulo alikuwa Mfarisayo. Aliwatesa Wakristo. Baada ya kuwa Mkristo, alisafiri mara kadhaa katika Ufalme wa Roma akiwaambia watu kuhusu Yesu.

Paulo alianzisha kanisa lililokutana huko Korintho. Alikuwa akiishi katika mji wa Efeso wakati aliandika barua hii.

Je, kitabu cha 1 Wakorintho kinahusu nini?

1 Wakorintho ni barua ambayo Paulo aliwaandikia waumini waliokuwa katika mji wa Korintho. Paulo alikuwa amesikia kwamba kuna matatizo kati ya waumini huko. Walikuwa wakigombana. Baadhi yao hawakuelewa baadhi ya mafundisho ya Kikristo. Na baadhi yao walikuwa na tabia mbaya. Katika barua hii, Paulo aliwajibu na kuwahimiza kuishi kwa njia iliyopendeza Mungu.

Je, kichwa cha kitabu hiki kinapaswa kutafsiriwaje?

Watafsiri wanaweza kuchagua kuita kitabu hiki kwa kichwa chake cha jadi, "Wakorintho wa Kwanza." Au wanaweza kuchagua kichwa wazi, kama "Barua ya kwanza ya Paulo kwa Kanisa la Korintho." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-names)

Sehemu ya 2: Dhana muhimu za Kidini na za Kitamaduni

Mji wa Korintho ulikuwaje?

Korintho ilikuwa mji mkuu katika Ugiriki wa kale. Kwa sababu ulikuwa karibu na Bahari ya Mediterane, wasafiri wengi na wafanyabiashara walikuja kununua na kuuza bidhaa huko. Hii ilisababisha mji kuwa na watu kutoka tamaduni nyingi tofauti. Mji huo ulijulikana kwa kuwa na watu waliokuwa wameishi katika njia za uasherati. Watu waliabudu Afrodito, mungu wa kike wa Kigiriki wa upendo. Kama sehemu ya sherehe za kuheshimu Afrodito, waabudu wake walifanya ngono na makahaba wa hekalu.

Tatizo lilikuwa nini kwa nyama iliyotolewa kwa sanamu?

Wanyama wengi waliuawa na kutolewa dhabihu kwa miungu ya uongo huko Korintho. Wakuhani na waabudu walishika sehemu ya nyama hizo. Sehemu kubwa ya nyama hizo ilikuwa ikiuzwa katika masoko. Wakristo wengi hawakukubaliana iwapo ilikuwa ni sawa kula nyama hii, kwa sababu ilikuwa imetolewa kwa mungu wa uwongo. Paulo anaandika juu ya shida hii katika 1 Wakorintho.

Sehemu ya 3: Masuala muhimu ya Tafsiri

Je, mawazo ya "takatifu" na "kutakasa" yamewakilishwa vipi katika 1 Wakorintho kwenye ULB?

Maandiko hutumia maneno kama haya ili kuonyesha moja kati ya mawazo mbalimbali. Kwa sababu hii, mara nyingi ni vigumu kwa watafsiri kuyawakilisha vizuri katika tafsiri zao. Katika kutafsiri kwa Kiingereza, 1 Wakorintho kwenye ULB hutumia kanuni zifuatazo:

UDB mara nyingi husaidia ikiwa wafasiri wanafikiria juu ya jinsi ya kuwakilisha mawazo haya katika tafsiri zao wenyewe.

Nini maana ya "mwili"?

Paulo mara nyingi alitumia maneno "mwili" au "kimwili" kwa kutaja Wakristo ambao walifanya mambo ya dhambi. Hata hivyo, sio ulimwengu wa kimwili ambao ni mbaya. Paulo pia alielezea Wakristo ambao waliishi kwa njia ya haki kama "kiroho." Hii ni kwa sababu walifanya kile Roho Mtakatifu aliwafundisha kufanya. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#flesh, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#spirit)

Paulo alimaanisha nini kwa maneno "katika Kristo," "katika Bwana," na kadhalika?

Maneno haya hutokea katika 1:2, 30, 31; 3:1; 4:10, 15, 17; 6:11, 19; 7:22; 9:1, 2; 11:11, 25; 12: 3, 9, 13, 18, 25; 14:16; 15:18, 19, 22, 31, 58; 16:19, 24. Paulo alijaribu kueleza wazo la muungano wa karibu kati ya Kristo na waumini. Wakati huo huo, mara nyingi alitaka kuelezea maana nyingine pia. Ona, kwa mfano, "wale ambao wamejitolea katika Kristo Yesu" (1:2), ambako Paulo alimaanisha hasa kwamba waumini Wakristo wamejitolea kwa Kristo.

Tafadhali angalia utangulizi wa Kitabu cha Warumi kwa maelezo zaidi juu ya maneno haya.

Je, ni masuala gani muhimu katika Kitabu cha 1 Wakorintho?

Kwa aya zifuatazo, matoleo ya kisasa ya Biblia yanatofautiana na matoleo ya zamani. Watafsiri wanashauriwa kufuata matoleo ya kisasa ya Biblia. Hata hivyo, ikiwa katika wilaya ya watafsiri kuna Biblia ambazo zinasomwa kulingana na matoleo ya kale ya Biblia, watafsiri wanaweza kufuata hayo. Ikiwa ni hivyo, mistari hii inapaswa kuwekwa ndani ya mabano ya mraba ([]) ili kuonyesha kwamba labda asili yao sio 1 Wakorintho.

(See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/jit.html#translate-textvariants)

1 Corinthians 1

1 Wakorintho 01 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Aya tatu za kwanza ni salamu. Katika inchi za kale za Mashariki ya Karibu, hii ilikuwa njia ya kawaida ya kuanzisha barua.

Baadhi ya tafsiri huweka kila mstari wa mashairi upande wa kulia zaidi kuliko maandiko yote ili iwe rahisi kusoma. ULB hufanya hivi kwa maneno ya mstari wa 19, ambayo yanayotoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

Mgongano

Katika sura hii, Paulo anakaripia kanisa kwa kugawanyika na kwa kufuata mitume tofauti. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#apostle)

Vipaji vya kiroho

Vipaji vya kiroho ni uwezo usio wa kawaida wa kusaidia kanisa. Roho Mtakatifu anatoa vipaji hivi kwa Wakristo baada ya kumwamini Yesu. Paulo anaorodhesha vipaji vya kiroho katika Sura ya 12. Wasomi wengine wanaamini kwamba Roho Mtakatifu alitoa baadhi ya vipaji hivi katika kanisa la kwanza tu ili kusaidia kuanzisha kanisa. Wasomi wengine wanaamini kwamba vipaji vyote vya Roho bado vinapatikana ili kuwasaidia Wakristo wote katika historia ya kanisa. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith)

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Misemo

Katika sura hii, Paulo anaelezea kurudi kwa Kristo kwa kutumia maneno mawili tofauti: "ufunuo wa Bwana wetu Yesu Kristo" na "siku ya Bwana wetu Yesu Kristo." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-idiom)

Maswali ya uhuishaji

Paulo hutumia maswali ya uhuishaji ili kuwakaripia Wakorintho kwa kugawanyika katika vikundi na kwa kutegemea hekima ya kibinadamu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-rquestion)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Kikwazo

Kikwazo ni mwamba ambamo watu wanajikwaa. Hapa ina maana kwamba Wayahudi wanaona vigumu kuamini kuwa Mungu alimruhusu Masihi wake kusulubiwa. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

| >>

1 Corinthians 1:1

sentesi unganishi

Paulo na Sosthenes wanato salamu za kwa waumini wa kanisa la Korintho

Maelezo ya Jumla

Maneno kama vile "ninyi" and "yanu" yanahusiana na wale ambao paulo aliwaandikia na alitumia kiwakilisha cha wingi.

Paulo...kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho

Hii ilikuwa ni namna ya mwandishi wa barua kujitambulisha kwa wasomaji wake : " mimi, Paulo niliwaandikia barua hii ninyi munaomwamini Mungu mlioko Korintho"

Sosthene ndugu yetu

Hii inaonesha kuwa Paulo na Wakorintho wanamfahamu vema Sosthene:" Sosthene ndugu yetu ambaye mimi na ninyi tunamfahamu"

wale ambao wamewekwa wakfu katika Yesu Kristo

Neno "kuwekwa wakfu" linamaana ya watu ambao Mungu amewapa kibali cha kumtukuza yeye. " hii ni kwa wale ambao Yesu Kristo amaewatenga kwa ajili ya Mungu" au " watu ambao Mungu amaewachukua na kuwatenga kwa ajili yake mwenyewe kwa wanamwamini Yesu Kristo"

ambao wameitwa kuwa watu watakatifu

Hii inaweza kuelezewa kwa kitenzi tendaji: " ambao Mungu amewaita kuwa watu watakatifu" kuna maana mbili zinazokubalika. 1) " wale ambao Mungu amewatenga kwa ajili yake mwenyewe" 2) wale ambao Mungu amewaita kujitenga na dhambi" au ambao Mungu amewaita wajitenge na matendo ya dhambi"

Bwana wao na wetu

Yesu ni Bwana kwa Paul na kwa Wakorintho na ni Bwana kwa makanisa yote na watu wote

1 Corinthians 1:4

Sentensi Unganishi

Paulo anaelezea mwenendo na ushirika wa waumini katika Krito wanaposubiri kurudi kwake mara ya pili

kwa sababu ya neema ya Mungu ambayo Kristo Yesu aliwapa

Paulo anazungumzia neema kana kwamba ni kitu chenye umbo ambacho Yesu amewapa wakristo kama zawadi. " hii ni kwa sababu Yesu amefanya iwezekane kwa Mungu kuwa mwema kwako"

Amewafanya kuwa matajiri

Yawezekana maana ni 1)"Kristo amekufanya wewe tajiri" au 2) "Mungu amekufanya wewe tajiri."

Amewafanya kuwa matajiri katika kila njia

inatumia lugha ya makazo kumaanisha" aliwafanya matajiri wenye baraka nyingi za rohoni"

katika usemi

Mungu amekupa uwezo wa kuwaambia na kuwashirikiwe wengine kuhusu ujumbe kwa namna mbalimbali.

pamoja maarifa yote.

Mungu amekuwezesha kuelewa ujumbe wake kwa namna mbalimbali.

ushuhuda kuhusu Kristo ya kwamba amethibitishwa kuwa kweli miongoni mwenu.

maneno haya yanaweza kumaanisha: 1) ninyi wenyewe mliona tulichokise kwenu kuhusu Kristo ilikuwa ni kweli 2) watu wengine walijifunza kwa kuona ninyi na sisi tunavyoishi katika Kristo.

1 Corinthians 1:7

Kwa hiyo

"Kama matokeo"

hampungukiwi karama za kiroho

"kuwa na kila uwezo wa rohoni"

Ufunuo wa Bwana wetu Yesu Kristo

Yawezekana maana ni 1)Wakati Mungu atakapo mfunua Bwana Yesu Kristo" au 2)"Wakati Bwana wetu Yesu Kristo atakapojidhihirisha yeye mwenyewe."

msilaumiwe

Kusiwepo sababu yoyote ya kulaumiwa na Mungu

Mungu ni mwaminifu

Mungu atatimiza jambo lolote ambalo ameahidi kufanya.

mwana wake

Ni cheo cha Yesu Kristo, yaani "Mwana wa Mungu"

1 Corinthians 1:10

sentensi unganishi

Paulo anawakumbusha waumini wa Korintho kwamba wanapaswa kuishi katika umoja na katika ujumbe wa msalaba wa Kristo, siyo ubatizo wa watu unaoleta wokovu.

kaka na dada zangu

Hii inamaana washirika wote wakristo, ikijumuisha wote wanawake na wanaume.

kwamba wote mkubali

" kuishi katika hali ya upatanifu na ushirikiano"

kwamba kusiwe na migawanyiko miongoni mwenu

" kusiwe na migawanyiko ya makundi makundi miongoni mwenu"

kwamba muungane pamoja katika nia moja na katika kusudi

" muishi katika hali ya umoja"

watu wa nyumba ya Kloe

Hii inahusu wanafamilia, wafanyakazi, na watu wengine ambao ni sehemu ya kaya ambayo Chloe ni mwanamke kiongozi.

kuna mgawanyiko unaoendelea miongoni mwenu

" kuna makundi yenye migogoro na kugombana kati yenu"

1 Corinthians 1:12

Kila mmoja wenu husema

Paulo anaelezea kwa ujumla tabia ya mgawanyiko

Je! Kristo amegawanyika?

Paulo ataka kuweka makazo kuhusu ukweli kwamba Kristo hajagawanyika lakini ni mmoja. "Haiwezekani kumgawanya Kristo katika namna mnayofanya."

Je! Paulo alisulubiwa kwa ajili yenu?

Paulo anapenda kuweka mkazo kwamba alikuwa Kristo aliyesulubiwa wala si Paulo au Apolo. " ni ni ukweli uliowazi kuwa hawakumuua Paulo pale msalabani kwa ajili ya wokovu wenu."

Mlibatizwa kwa jina la Paulo?

Paulo anaweka mkazo kwamba wote tunabatizwa katika jina la Kristo. " Na Watu hawakuwabatiza ninyi katika jina la Paulo."

1 Corinthians 1:14

Namshukuru Mungu

Paulo anafurahia kuwa hakuwabatiza watu wengi wa pale Korintho

sikumbatiza yeyote isipokuwa

"pekee"

Krispo

Alikuwa kiongozi wa sinagogi ambaye alibadilika kuwa Mkristo.

Gayo

Alisafiri pamoja na Mtume Paulo

Hii ilikuwa hivyo kwamba hakuna hata mmoja angesema kwamba mlibatizwa katika jina langu.

"Nilijizua katika kubatiza watu zaidi kwasababu niliogopa kwamba wange jivuna baadaye kwamba nimekwisha kuwabatiza wao."

Nyumba nzima ya Stephania

Hii inahusu wanafamilia na watumwa katika nyumba(kaya) mahali Stephania, mwanaume, na kiongozi wa kaya.

1 Corinthians 1:17

Kristo hakunituma mimi kubatiza

Hii inamaanisha kwamba ubatizo halikuwa lengo la msingi la Paulo katika huduma yake.

maneno ya hekima ya kibinadamu...msalaba wa Kristo usionekane kuwa kitu kisichokuwa na nguvu

Paulo anazungumza kwa " maneno ya hekima ya kibinadamu" ni kama vile walikuwa watu, na msalaba ulikuwa kama chombo, ambacho Yesu aliweka nguvu yake ndani ya chombo hicho. Hii ilimaanisha kuwa " maneno yanayotokana na hekima ya kibinadamu ... yasije kuondoa nguvu ya msalaba wa Kristo" au " maneno ya hekima ya kibinadamu... yasiwafanye watu washindwe kuamini ujumbe kuhusu Yesu na kuanza kujidhania kuwa wao ni wamuhimu zaidi kuliko Yesu.

1 Corinthians 1:18

Sentensi Unganishi

Paul anasisitiza Hekima ya Mungu dhidi ya hekima ya kibidamu

ujumbe wa msalaba

"Mahubiri kuhusu kusulubiwa"au "ujumbe kuhusu kufa kwa Kristo msalabani."

ni upuuzi

"haina maana" au "ni upumbavu"

Kwa wale wanaokufa

Hapa "kufa" inamaanisha hatua ya kifo cha kiroho.

ni nguvu ya Mungu

" Mungu anafanya kazi katika utu wetu wa ndani"

Nitaiharibu hekima ya wenye busara

" nitaharibu busara za watu" au " nitaifanya mipango ya watu wenye busara isifanikiwe kabisa"

1 Corinthians 1:20

Yuko wapi mtu mwenye busara?Yukowapi msomi? Yuko wapi mpingaji wa dunia hii?

Paulo anafafanua kwamba watu wenye busara ya kweli hawatapatikana popote. " ukiwalinganisha na busara inayopatikana kupitia Injili , hakuna watu wenye busara, hakuna wasomi, hakuna waleta hoja!"

Msomi

Ni mtu aliyefahamika kuwa na mafunzo ya hali ya juu.

Mpingaji

Ni mtu anayeleta hoja ya kupinga kulingana na anachojua au ni mtu mweye ujuzi wa kufanya mabishano mbalimbali

Mungu hakuigeuza hekima ya dunia hii kuwa ujinga?

Paulo anatumia swali hili kufafanua kile Mungu amefanya kinyume na hekima ya dunia hii. "Mungu ameonesha kuwa kila kitu kilichokuwa ni hekima kwa watu kilikuwa ni upumbavu kabisa"

wale wanaoamini

Inaweza kumaanisha: 1)Wote wanaoamini ujumbe wa Injili" au 2)wote wanaoamini katika Kristo."

1 Corinthians 1:22

Maelezo kwa Ujumla

Hapa neno "sisi" linawakilisha Paulo na walimu wengine wa Biblia.

Kristo aliyesulubiwa

"Kuhusu Kristo, ambaye alikufa msalabani."

Kikwazo

Ni kama mtu anaweza kujikwaa juu yakizuizi barabarani, vile vile ujumbe wa wokovu kupitia kusulubiwa kwa Kristo ulikuwa kikwazo kwa Wayahudi wasiweze kuamini katika Yesu. "Kutopokelewa" au "Kikwazo sana"

1 Corinthians 1:24

kwa wale ambao waliitwa na Mungu

"Kwa watu walioitwa na Mungu"

Tunamhubiri Kristo

"Tuna fundisha kuhusu Kristo" au "Tunawaambia watu wote kuhusu habari za Kristo."

Kristo kama nguvu na hekima ya Mungu

Inaweza kumaanisha: 1) "Mungu alitenda kwa uweza na hekima kwa kumtuma Kristo kufa kwa ajili yetu" au 2) kupitia Kristo Mungu amethihilisha jinsi alivyo na nguvu na hekima.

nguvu...ya Mungu

Maana nyingine ni kwamba Kristo ni mwenye nguvu na kupitia Kristo, Mungu anatuokoa.

hekima ya Mungu

Maana nyingine ni kuwa Mungu aweka wazi hekima yake kupitia kwa Kristo

ujinga wa Mungu una hekima wanadamu, na udhaifu wa Mungu una nguvu zaidi ya wanadamu.

"kile ambacho watu huita upumbavu wa Mungu ni hekima ya kweli kuliko busara ya wanadamu, na kile watu huita udhaifu wa Mungu ni nguvu iliyo imara zaidi ya nguvu ya wanadamu"

1 Corinthians 1:26

Sentensi unganishi

paulo anasisitiza nafasi ya waumini Mbele za Mungu

Si wengi wenu

"Wachache tu kati yenu."

hekima katika viwango vya kibinadamu

"jambo linalokubalika kwa watu wengi kuwa ni busara"

mlizaliwa katika ukuu

"maalum kwa sababu familia yako ni muhimu" au '"kifalme"

Mungu alichagua vitu vijinga vya dunia ili kuviaibisha vyenye hekima

Mungu alichagua kutumia watu wanyenyekevu ambao viongozi wa Kiyahudi waliamini kuwa si muhimu kuthibitisha kwamba hawa viongozihawakuwa wa muhimu zaidikuliko wengine kwa Mungu.

Mungu alichagua kilicho dhaifu katika dunia kukiaibisha chenye nguvu

"Mungu aliwachagua wale ambao ulimwengu hufikiri ni dhaifu ili awaaibishe wale ambao ulimwengu hufikiri wapo imara"

1 Corinthians 1:28

hali ya chini na kilichodharauliwa

watu ambao dunia imewakataa."Watu ambao ni wanyenyekevu na kukataliwa."

Vitu ambavyo vimehesabiwa kuwa hakuna kitu

"Vile ambavyo watu kawaida huhesabiwa havithaminiwi"

vitu vilivyo na thamani

"Vitu ambavyo watu kwa kawaida huvithamini"au "Vitu ambavyo watu hudhani vina thamani au vinathaminiwa."

Alifanya hivi

"Mungu alifanya hivi"

1 Corinthians 1:30

Kwa sababu kile Mungu alichofanya

Hii inaonyesha kazi ya Kristo msalabani.

Sisi... yetu

Paulo anajumlisha wale waliotumika naye, pamoja na wakorintho

Kristo Yesu, ambaye amefanyika hekima kwa ajili yetu kutoka kwa Mungu

Hapa inaweza kumaanisha: 1) " Kristo Yesu aliyedhihirisha wazi kwetu jinsi Mungu alivyo wa Hekima" au 2) Kristo Yesu aliyetupatia Hekima ya Mungu"

Anayejisifu, ajisifu katika Bwana

"Kama mtu anajisifu, anapaswa kujisifu kuhusu jinsi Bwana alivyo mkuu."

1 Corinthians 2

1 Wakorintho 02 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri huweka kila mstari wa mashairi upande wa kulia zaidi kuliko maandiko yote ili iwe rahisi kusoma. ULB hufanya hivi kwa maneno ya mistari ya 9 na 16, ambayo yanatoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

Hekima

Paulo anaendeleza majadiliano kutoka sura ya kwanza ambayo yanalinganisha hekima ya binadamu na hekima ya Mungu. Kwa Paulo, hekima inaweza kuwa rahisi na mawazo ya kibinadamu kuwa pumbavu. Alisema hekima kutoka kwa Roho Mtakatifu ndiyo hekima pekee ya kweli. Paulo anatumia neno "hekima iliyofichwa" wakati anapozungumzia ukweli uliojulikana hapo awali. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#wise and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#foolish)

<< | >>

1 Corinthians 2:1

Sentensi Unganishi

Paulo anatofautisha kati ya hekima ya kibinadamu na hekima ya Mungu. anaeka mkazo kuwa hekima ya kiroho hutoka kwa Mungu.

kaka na dada zangu

Hii inamaanisha washirika wote(wakristo), wanaume na wanawake.

Niliamua kutojua chochote...isipokuwa Yesu Kristo

Paulo alilenga katika kusulubiwa kwa Kristo badala ya mawazo ya kibinandamu: " niliamua kuzungumza zaidi... kuhusu Kristo Yesu

1 Corinthians 2:3

Nilikuwa pamoja nanyi

"Nili kuwa nina watembelea

Katika udhaifu

Inawezekana maana ni 1) "udhaifu wa kimwili" au 2) "Kujisikia kupungukiwa."

maneno ya ushawishi

Ni maneno yanayoonekana kuwa ya busara, na msemaji anategemea watu wafanye anachosema au waamini.

1 Corinthians 2:6

Maelezo ya Jumla

Paulo anaanza kufafanuao hoja yake, kwamba anaposema hekima anamaana gani kwa wasomaji wake.

Sasa tunaizungumza

Neno "sasa" limetumiwa hapa kama alama ya kuonesha fundisho kuu. Paulo anaelezea kuwa hekima ya kweli ni ile hekima ya Mungu.

watu wazima

"Waumini walikomaa kiimani"

kabla ya nyakati

" Kabla Mungu hajaumba chochote"

za utukufu wetu

" ili kudhibitisha ujio wa kutukuzwa kwetu"

1 Corinthians 2:8

Bwana wa utukufu

"Yesu, Bwana wa utukufu."

Mambo ambayo hakuna macho...hayakufikiri, mambo ambayo ...wampendao Mungu

Inataja sehemu tatu za mwili wa mtu kumaanisha kwamba hakuna mtu aliyekwisha kuwa na ufahamu wa kina kwa vitu ambavyo Mungu ameandaa.

Mambo mbayo hakuna jicho limeyaona, hakuna sikio lililoyasikia, mawazo hayakufikiri

Inataja sehemu tatu za mwili wa mtu kumaanisha kwamba hakuna mtu aliyekwisha kuwa na ufahamu wa kina kwa vitu ambavyo Mungu ameandaa.

Vitu vile Mungu amekwisha andaa kwa wale wanampenda yeye.

Bwana amekwisha umba mbinguni vitu vya ajabu kwa wote wanaompenda yeye.

1 Corinthians 2:10

Hivi ni vitu

Paulo anazunguza kuhusu uhalisia wa Yesu na msalaba. mambo ambayo hakuyaeleza kwa kina 2:8 anayafafanua sasa.

Nani ajuaye mawazo ya mtu isipokuwa ni roho ya mtu katika yeye?

Paulo alitumia swali kufafanua kwamba hakuna yeyote ajuaye ni nini mtu anawaza isipokuwa mtu mwenyewe. "Hakuna yeyoteajuaye ni nini mtu anawaza isipokuwa roho ya mtu."

Roho ya mtu

Hii inaonyesha ndani ya mtu,asili ya kiroho yeye

Hakuna yeyote ajuaye vitu vya ndani ya Mungu isipokuwaRoho wa Mungu

"Roho wa Mungutu ajuaye vitu vya ndani ya Mungu"

1 Corinthians 2:12

Maelezo ya Jumla

Hapa "sisi" inajumlisha Paulo na wasikilizaji wake.

tuliyopewa na Mungu

"Kwamba Mungu alitupatia bure " au "kwamba Mungu ametupa kabisa bila malipo"

Roho hutafasiri maneno ya kiroho kwa hekima ya kiroho

Roho Mtakatifu huwasiliana kweli wa Mungu kwa waumini katika maneno ya rohoyenyewew na hutupa yenyewe hekima yake yenyewe.

hutafasiri

"fafanua"

1 Corinthians 2:14

Maelezo ya jumla

hapa neno "sisi" linajumuisha Paulo pamoja hadhira (watu anaowaandikia)

Mtu si wa kiroho

Mtu asiye mkristo,ambaye bado hajapokea Roho Mtakatifu.

yanatambuliwa kiroho.

"Kwa sababu kufahamu mambo haya kuanatokana na msaada wa Roho"

Kwa yule wa kiroho

"Muumini, aliyepokea Roho"

Ni nani anaweza kuyajua mawazo ya Bwana, ambaye anaweza kumfundisha yeye?

Paulo alitumia hili swali kufafanua kwamba hakuna yeyote ajuaye mawazo ya Bwana. "Hakuna yeyote anaweza kujua mawazo ya Bwana.Hivyo hakuna yeyote anaweza kumfundisha Bwana kitu chochote ambacho hakukifahamu kabla."

1 Corinthians 3

1 Wakorintho 03 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri huweka nukuu kutoka kwa Agano la Kale upande wa kulia zaidi kwenye ukurasa ili iwe rahisi kusoma. ULB inafanya hivyo kwa maneno yaliyotajwa kwenye mistari ya 19 na 20.

Dhana maalum katika sura hii

Watu wa kimwili

Waumini wa Korintho walikuwa hawajakomaa kwa sababu ya vitendo vyao vibaya. Anawaita "wa kimwili," maana matendo yao ni kama ya wasioamini. Neno hili linatumika kwa kinyume na wale ambao ni wa "kiroho." Wakristo wanaofuata "mwili" wao wanatenda upumbavu. Wao wanafuata hekima ya ulimwengu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#flesh, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#spirit and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#foolish and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#wise)

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Mifano

Kuna mifano nyingi katika sura hii. Paulo anatumia "watoto" na "maziwa" ili kuonyesha kutokomaa kwa kiroho. Anatumia mifano nyingi na kumwagilia maji ili kuelezea majukumu yake na Apolo katika kukuza kanisa la Korintho. Paulo anatumia mifano mingine katika kusaidia kufundisha ukweli wa kiroho kwa Wakorintho na kuwasaidia kuelewa mafundisho yake. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

<< | >>

1 Corinthians 3:1

Sentensi Unganishi

Paulo sasa anawakumbusha waumini wa Korintho juu maisha yao halisi badala ya kuishi kwa kujiheshimu kuzingatia nafasi yao mbele za Mungu. pia anawakumbusha kuwa mtu anayewapa mafundishi hawezi kuwa na unuhimu kama Mungu ambaye anawawezesha kukua.

kaka na dada zangu

hii inamaanisha washirika wote(wakristo) wanaume na wanawake

Watu wa kiroho

Watu wanaoishi kwa kumtii Roho

Watu wa mwilini

Watu ambao hufuata matakwa yao wenyewe

Kama watoto wachanga katika Kristo

Wakorintho wanalinganishwa na watoto wachanga katika umri na katika ufahamu. "Kama waumini wachanga katika Kristo"

Niliwanywesha maziwa na siyo nyama

Wakorintho wanaweza kuelewa mafundisho rahisi kama watoto wachanga ambao wanaweza kunywa maziwa tu. Hawajawa watu wazima kuelewa mafundisho ya kina kama watoto wakubwa ambao sasa wanaweza kula chakula kigumu.

Hamko tayari

"Hamko tayari kuelewa mafundisho magumu kuhusu kumfuata Kristo."

1 Corinthians 3:3

Bado wa mwilini

bado wanatabia ya dhambi au wanamatamanio ya kidunia

hamuishi kulingana na mwili, na je, hamtembei kama kawaida ya kibinadamu?

Paulo alikuwa anawaonya wakorintho kwa tabia zao za dhambi. "Mnapaswa kuona aibu kwa sababu munaishi kwa kufuata tamaa zenu mbaya na munaishi kwa kufuata desturi za kibinadamu.

Hamuishi kwa kawaida ya kibinadamu?

Paulo alikuwa anawaonya wakorintho kwa tabia zao za dhambi. "Mnapaswa kuona aibu kwa sababu munaishi kwa namna ileile wanayoishi watu wasio na Roho.

Apolo ni nani? Na Paulo ni nani?

Paulo alikuwa anafafanua kwamba yeye na Apolo hawakuwa chanzo cha injili na ndipo hawastahiri kufuatwa. "Ni mbaya kuunda makundi kufuata Apolo au Paulo!"

Paulo ni nani?

Paulo anaongelea habari zake mwenyewe kana kwamba anazungumzia habari za mtu mwingine. ni kama vile anauliza: "mimi ni nani?" au anasema "mimi siyo wa muhimu!"

Watumishi wa yule mliyemwamini

Paulo ajibu swali lake kwa kusema kwamba yeye na Apolo ni watumishi wa Mungu. "Paulo na Apolo ni watumishi wa Kristo, na mmeamini katika Kristo kwa sababu tunamtumikia yeye".

mliyemwamini, kwa kila ambaye Bwana alimpa jukumu.

" Sisi ni watu tu wa Bwanamuliyemwamini ambaye ametupatia majukumu."

1 Corinthians 3:6

Nilipanda

Ufahamu wa neno la Mungu unalinganishwa na mbegu ambayo lazima iwe imepandwa ili istawi

akatia maji

Kama vile mbegu huhitaji maji,imani inahitaji mafundisho zaidi ili iweze kukua.

Kukua

Kama mmea hukua na kuendelea,pia imani na ufahamu katika Mungu hukua nakuwa na kuwa na kina na uimara.

Kwa hiyo, si aliye panda ... anachochote. Lakini ni Mungu anayekuza.

Paulo anaeleza kwamba si yeye wala Apolo aliye nawajibu kwa ajili yakukua kiroho kwa wakristo, lakini ni utendajiwa Mungu.

anayekuza.

Paulo anaelezea kwa kielelezo cha ukuaji wa miti kuhusu ukuaji wa imani ya Wakoritho. : Anawezasha miti kukua" au " Mungu huwawezesha wakristo kumfahamu na kumjua Yeye kwa undani"

1 Corinthians 3:8

Anayepandana anayemwagilia ni sawa

Upandaji na umwagiliaji maji inahesabika ni kazi moja,ambayo Paulo analinganisha yeye mwenyewe na Apolo katika kuwahudumia kanisa la Wakorintho.

Ujira

Kiasi cha fedha ambacho mfanyakazi analipwa, kinalinganishwa kwa kiasi gani alichofanya kazi.

Sisi

Hii inaonyesha kwa Paulo na Apololakini si kanisa la Korintho

Wafanyakazi ya Mungu

Paulo anajitambulisha yeye na Apolo kuwa ni watendakazi pamoja.

bustani ya Mungu

Mungu anawajali waumini wa Korintho, Kama vile mtu ahudumiaye bustani yake ili kuzalisha matunda.

Jengo la Mungu

Mungu amewafanyia usanifuna kuwaumba waumini wa Korintho,kama vile mtu anayejenga jengo.

1 Corinthians 3:10

Kulingana na neemaya Mungu ambayo nimepewa

"Kulingana na uwezo ambao Mungu kweli amenipa kufanya."

Niliweka msingi

Paulo alianzisha mafundisho yake ya imani na wokovu katika Yesu Kristo, hii ilikuwa kama kuweka msingi wa jengo.

Mwingine anajenga juu yake

Paulo anamzungumzia mtu au watu wanaowafundisha Wakorintho kuwa kama maseremala wanaofanya ujenzi juu ya msingi aliokwisha kuujenga.

Kila mtu

Hii inaonyesha kwa wafanyakazi wa Mungu kwa ujumla. "Kila mtu anayemtumikia Mungu."

Hakuna mwingineanaweza kuanzisha msingi mwingine zaidi ya ule ambao umekwisha anzishwa.

hii inaweza kumaanisha " Tayari nimekwisha anzisha msingi ambao yeyote anaweza kujenga" au " hakuna awezaye kujenga Msingi zaidi ya ule niliojenga mimi, Paulo"

1 Corinthians 3:12

Maelezo ya Jumla

Paulo anazungumzia shughuli ambazo wajenzi hufanya wanapojenga jengo akifananisha na kile wanachofanya walimu wa Korintho. Wjenzi mara nyingi hutumia dhahabu, fedha, au mawe ya thamani kama mapambo ya majengo.

Sasa kamayeyote anajengajuu ya msingi kwa dhahabu,fedha, mawe ya thamani, miti,manyasi, au majani

Vitu vya ujenzi yamelinganishwa na thamani ya kiroho yatumikayo kwa kujenga tabia ya mtu na shughuli wakati wa maisha yake. "Hata mtu anajenga kwa thamani, vitu vya kudumu au vya chini,vitu vya kung'aa."

Mawe ya thamani

"Mawe ya gharama kubwa"

Kaziyake itafunuliwa

" Mungu ataweka wazi kila kazi aliyoifanya mjenzi."

kwa mwanga wa mchana utaidhihirisha

Neno "mwanga" ni sitiari kumaanisha wakati Mungu atakapomuhukumu kila mtu. Mungu atakapo weka wazi mafundisho ya walimu hawa, itakuwa kama nuru ya jua juu ya giza la usiku.

Kwa kuwa itadhihirishwa na moto. Moto utajaribu ubora wa kazi wa kila mmoja alichofanya.

Kama moto utadhihirisha uimara au kuharibu udhaifu wa jengo,Moto wa Mungu utahukumu juhudi ya mtu na shughuli. "moto utaonyesha thamani ya kazi yake."

1 Corinthians 3:14

Maelezo ya Jumla

Maneno "mtu" , "chochote mtu" "yeye" na " yeye mwenyewe" yanahusiana na washirika( waumini)

kitabaki

"Salia" au "kubakia"

Kama kazi ya mtu itateketea

"Kama moto utaharibu kazi ya mtu yeyote" au "Kama moto utahapoteza kazi ya mtu yeyote."

Yeyote...yeye...mwenyewe

Haya maneno yanaonyesha "mtu""mtu" au "yeye"

Atapata hasara.Lakini yeye mwenyewe ataokolewa

"Atapoteza kazi ile na tuzo yoyote anaweza kupata kama kazi ile itastahimili katika moto, lakini Mungu atamwokoa."

1 Corinthians 3:16

Hamjuwi kuwa ninyi ni hekalu la Mungu na kwamba Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?

Paulo anawakalipia Wakorintho: "Mnafanya kana kwamba hamjui kuwa ninyi ni hekalu la Mungu na Roho wa Mungu anakaa ndani yenu!"

Haribu

"haribu" au "hasara"

Mungu atamharibu mtu yule,Kwan hekalu la Mungu ni takatifu, na ni ninyi.

"Mungu atamharibu mtu yule kwasababu hekalu la Mungu ni takatifu na ninyi ni watakatifu piaa."

1 Corinthians 3:18

Mtu asijisifu mwenyewe

Mtu yeyote hanapaswa kuamini kwa kujidanyanya mwenyewe kwamba ni mwenye hekima katika ulimwengu huu.

Nyakati hizi

hii inahusu namna ambavyo watu wasioamini hufanya maamuzi

awe kama "mjinga"

"Yule mtu anapaswa kukubali kile ulimwengu hufikiri ni ujinga kwa ajili ya kupata hekima ya kweli ya Mungu"

Huwanasa wenye hekima kwa hila zao

Mungu huwatega watu ambao wanafikiri kuwa wana akili na anatumia mipango yao kuwatega wao

Bwana anajua mawazo ya wenye busara ni ubatili

"Bwana anajua kwamba mipango ya watu ambao hufikiri wana busara ni" au "Bwana anaelewa mipango yote ya wenyebusara na anajua yote ilivyo."

ubatili

"hayatumiki" "hakuna thamani"au "Hakuna pointi"

1 Corinthians 3:21

ninyi ni wa Kristo na Kristo ni wa Mungu

" Ninyi ni mali ya Kristo na Kristo ni mali ya Mungu"

1 Corinthians 4

1 Wakorintho 04 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Kiburi

Paulo analinganisha Wakorintho walio na kiburi na mitume walio wanyenyekevu. Waumini wa Korintho hawakuwa na sababu ya kuwa na kiburi. Yote waliyokuwa nayo, na waliyokuwa; yalikuwa zawadi kutoka kwa Mungu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#apostle)

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Mifano

Paulo anatumia mifano nyingi katika sura hii. Anaelezea mitume kama watumishi. Paulo anazungumza juu ya gwaride la ushindi ambapo mitume watakuwa ni wafungwa ambao watauawa. Anatumia fimbo ili kumaanisha adhabu. Anajiita baba yao kwa sababu yeye ni "baba yao wa kiroho." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#spirit)

Kinaya

Paulo anatumia kinaya kuwaaibisha Wakorintho kwa kuwa na kiburi. Waumini wa Korintho wanatawala lakini mitume wanateseka. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-irony)

Maswali ya uhuishaji

Paulo anatumia maswali kadhaa ya uhuishaji katika sura hii. Anayatumia kusisitiza neno muhimu anapofundisha Wakorintho. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-rquestion)

<< | >>

1 Corinthians 4:1

sentensi unganishi

baada ya kuwakumbusha watu kuwa wasiwe na majivuno juu ya nani aliwafundisha habari za Bwana na kuwabatiza, pia anawakumbusha washirika(waumini) wa Korintho kuwa wanapaswa kuwa wanyenyekevu.

Katika hili

"Kwa sababu sisi ni mawakili"

kinachotakiwa kwa uwakili ni kwamba wawe

" tunatakiwa kuwa"

1 Corinthians 4:3

Ni kitu dogo sana kuwa ninahukumiwa na ninyi

Paulo analinganisha kati ya hukumu ya kibinadamu na hukumu ya Mungu. Hukumu ya binadamu ni ya kubahatisha kulinganisha na hukumu ya kweli ya Mungu juu ya binadamu

Sijihukumu mimi mwenyewe

"Sijasikia lawama yoyote juu yangu kwamba nilifanya maovu"

hii haina maana kuwa mimi ni mwenye haki. Ni Bwana anihukumuye

"kule kutosikia lawama siyo uthibitisho kuwa mimi sina hatia. Bwana anajua kama mimi sina hatia au nina hatia.

1 Corinthians 4:5

Kwa hiyo,msitamke hukumu

Kwa kuwa Mungu atahukumu atakaporudi, tusihukumu.

atayaleta nuruni mambo yaliyofichika gizani na kufunua makusudi ya mioyo

Mungu ataweka wazi mawazo na dhamira za watu. Hakuna kitakachofichika mbele za Bwana.

ya mioyo

"ya mioyo ya watu"

1 Corinthians 4:6

kaka na dada zangu

Hii inamaanisha washirika/ wakristo (waumini)wote wanaume na wanawake

kwa ajili yenu

"kwa ajili ya ustawi wenu, au mafaa yenu"

tofauti kati yenu...Ni nini ulicho nacho hukukipokea... kupokea bure, kwa nini mnajivuna kama hamkufanya hivyo

Paulo anawaongelea Wakorintho kana kwamba anazumgumza na mtu mmoja, ndiyo maana katika matukio yote anatumia kiwakilishi cha "wewe".

ni nani aonaye tofauti kati yenu na mwingine?

Paulo aliwaonya Wakorintho ambao wanafikiri wao ni bora kwa kuwa wameamini injili kwa Paulo au kwa Apolo. "Hamko bora zaidi ya watu wengine."

Ni nini ulicho nacho hukukipokea bure?

Paulo alieleza kwamba Mungu aliwapa kile walicho nacho kwa bure. "Kila kitu mlichonacho, Mungu amewapa bure, bila malipo yoyote!"

Kwa nini mnajivuna kama hamkufanya hivyo?

Paulo alikuwa anawaonya kwa kujivuna kwa kile walichopokea. "Hamna haki ya kujivuna" au "Msijivune kabisa."

1 Corinthians 4:8

Maelezo ya Jumla

Paulo anatumia msemo wa kejeli ili kuwafanya Wakorintho waone aibu na kutambua kuwa walikuwa wakitenda dhambi walipojisifu wenyewe pamoja na kuwasifia walimu wao.

Mungu ametuweka sisi mitume kama kutuonyesha

Paulo anaeleza njia mbili jinsi Mungu amekwisha weka mitume kwa kuonyesha wazi kwa ulimwengu uone

ametuweka sisi mitume kama kutuonyesha

Mungu ameonyesha wazi mitume kama tu wafungwa wakti wa mwisho wa gwaride la jeshi la Kirumi,ambao tunaabishwa mbele ya kutekeleza kwao.

kama watu waliohukumiwa kuuawa

Mungu ameweka mitume kuonyesha wazi kama watu waliotayari kutekelezwa.

kwa ulimwengu, kwa malaika na kwa wanadamu

Neno "ulimwengu" ni jumla ya viumbe vya kiroho (malaika) na viumbe vya asili (wanadamu). kwa hiyo anataja vitu vitatu: kwa ulimwengu, kwa malaika, na kwa wanadamu

1 Corinthians 4:10

Sisi tu wajinga kwaajili ya Kristo, lakini mna busara katika Kristo.

Paulo anatumia kinyume kutofautisha mtazamo wa dunia na mtazamo wa Kikristo wa kuamini katika Kristo.

Sisi ni wadhaifu, lakini ninyi mna nguvu

Paulo anatumia kinyume kutofautisha mtazamo wa kidunia na mtazamo wa kikristo wa kuamini katika Kristo.

Mmeheshimiwa

"Watu wanawahesabu Wakorintho katika nafasi ya heshima."

Tunasika katika hali ya kutoheshiwa

"Watu wanatuhesabu sisi mitume katika nafasi ya kutoheshiwa."

Hata kwa saa hii iliyopo

"Mpaka sasa" au "Kufikia sasa"

Tumepigwa vibaya

"Adhibiwa kwa mapigo makaliya mwili"

1 Corinthians 4:12

Tunapodharauliwa, tunabariki

"Wakati watu wanapotudharau, sisi tunawabariki."

Dharau

"Beza"inawezekana "onea" au "laani"

Tunapoteswa

"Wakati watu wanapotutesa"

Tunapokashifiwa

"Wakati watu wanatukashifu"

Tumekwisha kuwa,na tunasubiriwa kuwa, kukataliwa na dunia

"Tumekuwa, na watu bado wanatusubiri kuwa, takataka za dunia."

1 Corinthians 4:14

Siandiki vitu hivi kuwaaibisha ninyi, lakini kuwarudi ninyi

Sifanyi kuwaaibisha, lakini kuwathibitisha" au Sijaribu kuwaaibisha, lakini nataka kuwarudi."

Sahihisha

"thibitisha"au "fanya bora"

Waalimu makumi elfu

Huu ni ukuzaji wa idadi ya watu wanao waongoza,Kuelezea umuhimu wa wa baba mmoja wa kiroho.

watoto...baba

Kwa sababu Paulo amewaongoza kwa Kristo,yeye ni kama baba kwa Wakorintho

sihi

"Kuwatia moyo kwa nguvu" au "Kuthibitisha kwa nguvu"

1 Corinthians 4:17

Sasa

Hili neno linaonyesha kwamba Paulo anabadilisha mada yake kwa kuwarudi wenye tabia ya majivuno walio waumini wa Korintho.

1 Corinthians 4:19

Nitakuja kwenu

"Nitawatembelea"

haitegemeikatika kusema

"haitendwi kwa maneno" au "Si nini usemacho"

Nini unachotaka?

Paulo alikuwa anawasihi kwa mwisho Wakorintho, kamaamekwisha warudi kwa makosa waliyokwishafanya. "Niambieni nini mnataka kitokee sasa."

Nije kwenu na fimbo au na upendo na roho ya upole.

Paulo anatoa tabia mbili tofauti kwa Wakorintho, atakazotumia atakapofika kwao. "Mnataka nije kuwafundisha ninyi kwa lazima, au mnataka nionyeshe upendo na kwa upole?"

upole

"wema au "uzuri"

1 Corinthians 5

1 Wakorintho 05 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri huweka nukuu kutoka kwa Agano la Kale upande wa kulia zaidi kwenye ukurasa ili iwe rahisi kusoma. ULB inafanya hivyo kwa maneno yaliyotajwa kwenye mstari wa 13.

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Maneno ya badla ya kupunguza uzito

Paulo anatumia maneno ya rahisi ya kupunguza uzito kuelezea mada nyeti. Sura hii inahusika na uasherati wa kijinsia wa mwanachama mmoja wa kanisa. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-euphemism and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#fornication)

Mfano

Paulo anatumia ulinganisho uliopanuliwa kwa kutumia sitiari nyingi. Chachu inawakilisha uovu. Mkate labda inawakilisha kanisa nzima. Mikate isiyotiwa chachu inawakilisha kuishi kwa utakatifu. Basi kifungu hiki kina maana: Je, hujui kwamba uovu mdogo utaathiri kanisa lote? Hivyo basi uondoe uovu huu ili uweze kuishi kwa utakatifu. Kristo ametolewa kama sadaka kwa ajili yetu. Kwa hiyo tuwe waaminifu na wa kweli na sio waovu na wanaofanya mabaya. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#evil, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#unleavenedbread and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#purify and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#passover)

Maswali ya uhuishaji

Paulo anatumia maswali ya uhuishaji katika sura hii. Anayatumia ili kusisitiza maneno muhimu anapofundisha Wakorintho. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-rquestion)

<< | >>

1 Corinthians 5:1

Sentensi Unganishi

Paulo anaelezea kwa ufasaha kwamba amesikia kuna dhambi miongoni mwa waumini wa Wakorintho, na namna Wakorintho walivyojisifu na kukaa pamoja na mtu aliyetenda ile dhambi.

Ile hairuhusiwi hata miongoni mwa mataifa

Katika muundo tendaji " hata watu wa wasioamini hawawezi kuruhusu"

Mke wa baba

mke wa baba yake, lakini yawezekana si mama yake wa kumza

Hampaswi kuhuzunika badala?

Hili ni swali lenye jibu limetumika kuwakemea Wakorintho. "Mnapaswa kuhuzunika kwa hili jambo!"

Yeye aliyefanya hivi lazima awe ameondolewa miongoni mwenu

Katika hali ya muundo tendaji:- "Ni lazima aondolewe miongoni mwenu aliyefanya jambo hili ."

1 Corinthians 5:3

...nipo nanyi kiroho

"... kila wakati nafikiri juu yenu."

nimekwisha mhukumu yeye aliyefanya hivi

"Nimekwisha ona huyu mtu ana hatia"

Mnapokutanika pamoja

"kutana"

katika jina la Bwana Yesu

lugha ya kuelezea tendo la kukusanyika pamoja kumwabudu Yesu Kristo

Nimekwisha

" tayari nimemhukumu mtu huyo"

kumkabidhi mtu huyu kwa Shetani

Hii inaonyesha kumfukuza mtu kutoka kwa watu wa Mungu,ili aishi katika utawala wa Shetani, ulimwengu nje ya Kanisa.

ili kwamba mwili wake uharibiwe

ili kwamba mwili wa mtu huyo upate maradhi kwa kurudiwa na Mungu kwa dhambi yake

1 Corinthians 5:6

Majivuno yenu si kitu kizuri

"Majivuno yenu ni mabaya"

Hamjui chachu kidogo huharibu donge zima?

Kama hamira kidogo husambaa kwa mkate mzima, hivyo dhambi ndogo inaweza kuathiri ushirika wote wa waumini.

Kristo, Mwana Kondoo wetu wa pasaka amekwisha kuchinjwa

"Bwana Mungu amemtoa KristoYesu, mwanakondoo wetu wa Pasaka"

1 Corinthians 5:9

wazinzi

Hii inahusu watu wanaokiri kuamini katika Kristo lakini wana tabia mbaya.

Wazinzi wa dunia hii

Watu waliochagua kuishi katika maisha uzinzi,ambao si waumini

wenye tamaa

"Wale walio na tamaa" au "Wale waliotayari kupoteza heshima ili kupata kitu wanchotamani"

Wanyang'anyi

Hii ina maana watu ambao"wanadanganya au tapeli mali za watu wengine"

basi ingewapasa mtoke duniani.

" ingeliwabidi kukaa mbali na watu wote"

1 Corinthians 5:11

Sentensi Unganishi

Paulo anawaambia namna ya kukaa na waumini waliopo kanisani ambao hawataki kukosolewa juu ya matendo yao ya zinaa na dhambi zilizo wazi kwa wengine.

yeyote aliyeitwa

" yeyote anayejiita mwenyewe"

Kaka au Dada

Hii inamaanisha mshirika katika ukristo ama wanamke au mwanaume

Kwa hiyo nitajihusishaje kuwahukumu walio nje ya Kanisa?

Paulo anasisitiza kwamba yeye siyo hakimu wa watu walio nje ya kanisa. kwa maneno mengine "Sipaswi kutoa hukumu kwa watu ambao si wa kanisani"

ninyi hamkuwahukumu walio ndani ya kanisa?

"Mnapaswa kuwahukumu wale wako ndani ya kanisa."

1 Corinthians 6

1 Wakorintho 06 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Mashtaka

Paulo anafundisha kwamba Mkristo hapaswi kuchukua Mkristo mwingine kwa mahakamani mbele ya hakimu asiye Mkristo. Ni bora zaidi kudanganywa. Wakristo watawahukumu malaika. Kwa hiyo wanapaswa kuwa na uwezo wa kutatua matatizo kati yao wenyewe. Ni mbaya sana kutumia mahakama kumdanganya mwamini mwingine. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#judge)

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Mfano

Hekalu la Roho Mtakatifu ni mfano muhimu. Inaelezea mahali ambapo Roho Mtakatifu anakaa na kuabudiwa. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

Maswali ya uhuishaji

Paulo anatumia maswali kadhaa ya uhuishaji katika sura hii. Anayatumia kusisitiza manen muhimu anapofundisha Wakorintho. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-rquestion)

<< | >>

1 Corinthians 6:1

Sentensi Unganishi

Paulo anaelezea jinsi waumini wanavyoweza kusuruhisha migogoro miongoni mwao

Tatizo

"Kutokubaliana" au "Mabishano"

je anathubutu kwenda kwa mahakama ya dunia mbele ya hakimu asiyeamini, kuliko mbele ya waumini?

Paulo asema kwamba Wakristo lazima wamalize matatizo miongoni mwao wenyewe. " Asithubutu kwenda.... waumini" au " anapaswa kuwa na hofu ya Mungu na asiende...waumini!"

mahakama ya wasio haki

Ni sehemu ambapo hakimu wa serikali huamua kesi na kuamua nani aliye na haki.

Hamjuwi kwamba waumini watauhukumu ulimwengu?

Paulo anawafanya Wakoritho wapate aibu kwa kutenda kana kwamba hawajui

Kama mtauhukumu ulimwengu, hamuwezikuweka sawa mambo yasiyo ya muhimu?

Paulo anasema baadaye watapewa wajibu mkubwa, hivyo kwa sasa lazima kushughulikia haya maswala madogo. "Mtauhukumu ulimwengu wakati ujao, hivyo mnaweza kusuruhisha tatizo hili kwa sasa."

Je mnajui kwamba tutawahukumu malaika?

Paulo anashangaa maana wanaonekana hawajui "Mnajua kwamba tutawahukumu malaika."

Kwa kiasi gani zaidi, tunaweza kuamua mambo ya maisha haya?

"Kwa sababu tunajua kuwa tutawahukumu malaika, na katika maisha haya tunauhakika kuwa Mungu anauwezo wa kuhukuma mambo mbali mbali."

1 Corinthians 6:4

Kama tunaweza kuhukumu mambo ya maisha haya, kwa nini mnathubutu kupeleka mashitaka mbele ya wasiosimama kanisani?

Inaweza kumaanisha 1) hili ni swali lisilohitaji jibu au 2) hii ni sentensi " Mliwahi kusuruhisha migogoro inayohusu maswala ya muhimu maishani, hamkuruhusu matatizo ya Wakristo yasuruhishwe na wasioamini" au 3) Hii ni amri "mnaposuruhisha juu ya maswala muhimu ya maisha, pia suruhisheni migogoro ambayo ipo kanisani " "Kama umeitwa kufanya maamuzi kuhusu maisha ya kila siku." au "Kama una ulazima wa kuweka sawa mambo ambayo ni muhimu katika maisha haya."

Kama tunaweza kuhukumu mambo ya maisha haya

" kama mmeitwa kufanya maamuzi kwa maisha ya kila siku" au " kama mtasuruhisha maswala ya muhimu katika maisha haya"

kwa nini mnathubutu kupeleka mashitaka

" msipeleke mashitaka hayo"

mbele ya wasiosimama kanisani?

Maana zinazokubalika 1) " acheni kupeleka mashitaka hayo kwa watu walio nje ya kanisa" au 2) " mngeweza kupeleka mashitaka hayo hata kwa waumini wasioamika kwa waumini wenzao"

kwa aibu yenu

" kwa kukosa heshima" au "kwa kuonyesha kuwa mmeshindwa katika swala hili"

Hakuna mwenye busara miongoni mwenu wa kutosha kuweka mambo sawa kati ya ndugu na ndugu?

" mnapaswa kuona aibu kwamba hamuwezi kupata muumini wenye hekima kumaliza mibishano miongoni mwa waumini"

ndugu

hapa inamaanisha waumini wote

mashitaka

" mabishano" au " kushindwa kukubaliana"

Lakini kama ilivyo

" namna ilivyo sasa" au " lakini badala "

mwamini mmoja huenda mahakamani dhidi ya muumini mwingine, na mashitaka hayo huwekwa mbele ya hakimu asiyeamini!

" waumini wenye mgogoro wanaomba usuruhishi kwa mahakimu wasioamini kufanya maamuzi juu yao"

mashitaka hayo huwekwa

" muumini anapeleka mashitaka"

1 Corinthians 6:7

usumbufu

"shindwa" au "poteza"

Kwanini msumbuke kwa mabaya? Kwaninimruhusu ninyi wenyewe kudanganywa?

"Ni bora kuacha wengine kuwafanyia mabaya na kuwadanganya kuliko kuwapeleka mahakamani,"

kaka na dada zenu wenyewe

Waumini wote katika Kristo ni kaka na dada kwa kila mmoja. "Waumini wenzako"

1 Corinthians 6:9

Hamjui kwamba

Paulo anaelezea kwamba wanapaswa tayari kuwa wanaujua ukweli huu. "Tayari umejua vile"

Wasio haki hawatarithi

"wenye haki tu watarithi"

kurithi ufalmewa Mungu

Mungu hatawahukumu kama wenye haki katika hukumu, na hawataingia katika uzima wa milele.

Wafiraji

Hawa ni malaya ambao ni wanaume hulala na wanaume wengine.

Wale wanaofanya uzinzi

Wanaume ambao hulala na wanumewengine(Walawiti)

wenye tamaa

watu walio tayari kutumia njia mbaya kujipatia mali

wadhalimu

"matapeli"

mlisafishwa

Mungu amewasafisha

mliwekwa wakfu kwa Mungu

Mungu amewatenga kwa ajili yake.

Mmefanywa haki pamoja na Mungu

Mungu amewafanya haki pamoja na yeye

1 Corinthians 6:12

Sentensi Unganishi

Paulo anawakumbusha waumini wa Korintho kuwa Mungu anataka wawe watakatifu kwa sababu Kristo aliwanunu kwa kifo chake.

Kila kitu ni halali kwangu

Mungu ameniruhusu kufanya kila kitu.

lakini si kila kitu kina faida

Lakini si kila kitu ni kizuri kwangu

Sitatawaliwa na chochote kati hivyo

Sitaruhusu vitu hivi vinitawale

"Chakula ni kwa ajili ya tumbo, na tumbo ni kwa chakula," lakini Mungu atavitowesha vyote

""Wengine husema 'chakula ni kwa tumbo, na tumbo ni kwa chakula; ' lakini Mungu atavitowesha vyotetumbo na chakula"

kutowesha

"kuharibu"

1 Corinthians 6:14

alimfufua Bwana

sababisha Yesu kuishi tena

Hamjuwi kwamba miili yenu ni muunganiko wa Kristo?

Kama tu mikono na miguu ni muunganiko wa miili yetu. Hivyo miili yetu ni muunganiko na mwili wa Kristo- Kanisa. "Miili yenu ni kiungo cha Kristo"

Nitatoa muunganiko wa Kristo na kuungana kwa kahaba?

"Ninyi ni viungo vya Kristo.Sitawaunganisha kwa kahaba."

Haiwezekani!

"Haiwezi kamwe kutokea vile!"

1 Corinthians 6:16

Hamjui kwamba

" nataka niwakumbushe kuwa..."

anayeungana na kahaba amekuwa mwili mmoja naye

" mwanaume anayeunganisha mwili wake kwenye mwili wa kahaba , miili yao inakuwa mwili mmoja"

Lakini anayeungana na Kristo amekuwa roho moja na yeye

" Bwana anapounganisha roho yake kwenye roho ya mtu, roho zao zinakuwa roho moja."

1 Corinthians 6:18

Kimbieni

kukimbia kimwili kwa mtu kutoka kwa hatari kunafanishwa na kiroho kwa mtu kukataa dhambi. "Toka"

"Kila dhambi ambayo mtu hufanya ni nje ya mwili," lakini uzinzi mtu hutenda dhambi kinyume na mwili wake mwenyewe

Dhambi ya uzinzi ni mbaya kwa sababu ni dhambi dhidi ya mwili wa mtenda dhambi

hutenda

"kufanya tendo"

1 Corinthians 6:19

Hamjui...

Nataka niwakumbushe...

Mwili wako

Mwili wa kila Mkristo binafsi ni hekalu la Roho Mtakatifu

Hekalula roho Mtakatifu

Hekalu limewekwa wakfu kwa kusudi maalum, na pia ni mahali anapoishi. Katika njia moja, kila mwili wa muumini wa wakorintho ni kama hekalu, kwa sababu Roho Mtakatifu yupo pamoja nao.

Ninyi mlinunuliwa kwa thamani

Mungu amelipa kwa uhuru wa Wakorintho kutoka katika utumwa wa dhambi. "Mungu alilipa kwa uhuru wenu."

Kwa hiyo

"Hivyo" au "Kwa kuwa hii ni kweli" au "kwa sababu ya ukweli huu."

1 Corinthians 7

1 Wakorintho 07 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Paulo anaanza kujibu mfululizo wa maswali ambayo Wakorintho wanaweza kumwuliza. Swali la kwanza ni kuhusu ndoa. Swali la pili ni kuhusu mtumwa akijaribu kuwa huru, asiye Myahudi kuwa Myahudi, au Myahudi kuwa asiye Myahudi.

Dhana maalum katika sura hii

Talaka

Paulo anasema Wakristo walio katika ndoa hawapaswi kutaliki. Mkristo aliyeolewa na asiyeamini hapaswi kuacha mume au mke wake. Ikiwa mume au mke asiyeamini anaondoka, hii sio dhambi. Paulo anashauri kwamba, kwa sababu ya nyakati ngumu na kuwa muda ambapo Yesu atarudi umekaribia, inakubalika kutoolewa. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#believe and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Maneno ya rahisi ya kupunguza uzito

Paulo anatumia maneno ya rahisi ya kupunguza uzito kwa busara kutaja mahusiano ya ngono. Hii mara nyingi hii ni mada nyeti. Tamaduni nyingi hazitaki kuzungumza waziwazi kuhusu mambo haya. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-euphemism)

<< | >>

1 Corinthians 7:1

Sentensi Unganishi

Paulo anatoa maelekezo mahususi juu ya ndoa

Sasa

paulo anatambulisha mada mpya katika mafundisho yake

Vitu mlivyoandika kwangu

Wakorintho walikwisha andika barua kwa Paulo kuomba kupatiwa majibu kuhusu baadhi ya maswali.

kwa mwanaume

Hapa ina maanisha mwanume mwenzi au mme

Lakini kwa sababu ya majaribu kwa matendo mengi maovu

'Lakini kwa sababu Shetani anawajaribu watu kutenda dhambi ya uzinzi'

1 Corinthians 7:3

haki ya ndoa

Waume na wake wanawajibika kwa kawaida kulala na wenzi wao.

1 Corinthians 7:5

Msinyimane

"Msikatae kulala pamoja wenzi wenu"

Fanyeni hivyo ili kupata muda wa maombi

Ili mpate muda maalumu wa maombi.

Fanyeni hivyo

""Jikabidhi ninyi wenyewe"

kurudiana tena pamoja

"Lala pamoja tena"

Kwa sababu ya kukosa kujitawala wenyewe

tawala- "Kwa sababu baada ya siku, tamaa yako ya zinaa itakuwa ngumu zaidi kuitawala"

Ninasema vitu hivi kwenu zaidi kama hiari nasio kama amri

Hapa inamaanisha 1) kuoana na kulala pamoja 2) kuacha kulala pamoja kwa muda

kama mimi

Labda Paulo hakuwahi kuoa au mke wake alifariki.

Lakini kila mmoja na karama yake kutoka kwa Mungu.Mmoja ana aina hii ya karama, na mwingine karama ile.

Mungu anawawezesha watu kufanya mambo yanayotofautiana.

1 Corinthians 7:8

wasioolewa

Hawa ni wale ambao hawajaolewa.

wajane

" wanawake walifiwa na waume wao"

ni vizuri

Neno "Vizuri"hapa linaonyesha haki na kukubalika. "Ni haki na kukubalika"

kuwaka tamaa

"Kuishi kwa tamaa ya kutaka kulala na mtu fulani"

1 Corinthians 7:10

asitengane

Hakuna tofauti kati ya taraka na kutengana. kutengana ni kuacha kuishi pamoja

apatane na

"Anapaswa kutatua mambo yake pamoja na mme wake na kurudi kwake"

asimpe talaka

"haipaswi kuachana."

1 Corinthians 7:12

anaridhika

"utayari" au "utoshelevu"

Kwa mwanaume asiyeamini atakubaliwa

" Mungu amewakuli wanaume wasioamini"

Mwanamke asiyeamini atakubaliwa

"Mungu ameshamkubali mwanamke asiyeamini"

wamekubaliwa

"Mungu amekwisha wakubali"

1 Corinthians 7:15

Kesi kama hiyo,kaka au dadahafungwi katika viapo vyao.

Kwa kesi hiyo,ndoa ya aaminiye makubaliano hayaendelei"

Unajuaje, mwanamke anaweza kumwokoa mme wake?

"hujuwi kama utamwokoa mwanaume asiyeamini."

Unajuaje, mwanaume anaweza kumwoka mke wake

"Haujuwi kamautamwokoa mkewako asiyeamini."

1 Corinthians 7:17

Kila mmoja

"Kila muumini"

Hii ni kawaida kwa kila kanisa

Paulo alikuwa anafundisha waumini katika makanisa yote kufuata katika njia hii.

yeyote alikuwa ametahiriwa alipoitwa kuamini.

Paulo alikuwa anafikisha ujumbe utahiriaji(Wayahudi) "Kwa waliotahiriwa, Mungu alipowaita kuamini, Mlikuwa tayari mmetahiriwa."

Yeyote alipoitwa kwa imani alikuwa hajatahiriwa.

Paulo alikuwa sasa anafikisha ujumbe kwa wale walikuwa hawajatahiriwa. "Kwa waliokuwa hawajatahiriwa ,Mungu alipowaita kuamini, mlikuwa bado kutahiriwa."

1 Corinthians 7:20

Maelezo ya Jumla

mli..msi.. ni maneneo kuonyesha wingi, yanahusu wakristo wote.

katika wito

Hapa "wito"inaonyesha kwa kazi au nafasi ya jamii katika sehemu uliyokuwa unajihusisha. "ishi na fanya kazi kama ulivyofanya."

Ulikuwa mtumwa ulipoitwa na Mungu?

"Kwa wale amabao walikuwa watumwa walipoitwa na Mungu kuamini."

Mtu huru wa Bwana

Hii mtu huru ni mmesamehewa na Mungu and kwa hiyouhuru kutoka kwa Shetani na dhambi.

Mmeshanunuliwa kwa thamani

"Kristo amewanunuakwa kufa kwa ajili yenu"

Tulipoitwa kuamini

"Wakati Mungu alipotuita kuamini katika yeye"

1 Corinthians 7:25

Sasa kuhusu wote ambao hawajaoa kamwe, sina amri kutoka kwa Bwana

Paulo anajua si mafundisho ya Yesu yale anazungumza kuhusu hali hii."Sina amri kutoka kwa Bwanakuhusu watu ambao hawajoa kamwe."

nawapa maoni

Ninawaambia ninachofikiri.

Kwa hiyo

" Basi hayo ni mawazo yangu"

usumbufu

"Mahangaiko yanayokuja"

1 Corinthians 7:27

Umefungwa na mwanamke katika viapo vya ndoa

Paulo anawaambia wanaume ambao wameoa

Umefungwa kwa mwanamke na kiapo cha ndoa? Usitake

" kama umeoa usitafute"

Una uhuru kutoka kwa mke au hujaolewa?

" Kama hujaoa usitafute kuoa"

Usitafute mke

"Usijaribu kutafuta kuoa"

1 Corinthians 7:29

Muda ni mfupi

"Kuna wakati mfupi" au "Wakati umekwisha"

Huzuni

"Kulia" au "Kutoa machozi"

wote wanaoshughulika na ulimwengu

"Wale ambao wanashughulika kila siku na wasioamini"

wawe kama hawakushughulika nao

Hii ni kwa sababu utawala wa Shetani wa dunia hii utakoma kitambo.

1 Corinthians 7:32

huru kwa masumbufu yote

"tulia" au "kutokuwa na wasi wasi"

anajihusisha

"shughulika"

Amegawanyika

"Anajaribu kumpendeza Mungu na kumpendeza mke wake"

1 Corinthians 7:35

Mtego

"mzigo" au "Kizuizi"

wanaweza kudumu kwa

"weza kushughulikia"

1 Corinthians 7:39

Wakati anapoishi

"mpaka afe."

ambavyo apenda

"Yeyote ampendaye"

Katika Bwana

"Kama mme mpya ni mwamini"

Maamuziyangu

"ufahamu wangu wa Neno la Mungu"

Furaha zaidi

"Kuridhika zaidi, Furaha zaidi"

aishi kama alivyo

"baki bila kuolewa."

1 Corinthians 8

1 Wakorintho 08 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Katika Sura ya 8-10, Paulo anajibu swali hili: "Je, inakubalika kula nyama ambayo imetolewa dhabihu kwa sanamu?"

Dhana maalum katika sura hii

Nyama iliyotolewa dhabihu kwa sanamu

Paulo anajibu swali hili kwa kusema kwamba sanamu ni miungu ambayo haipo. Kwa hiyo hakuna ubaya wowote kwa hiyo nyama. Wakristo wana uhuru wa kula. Hata hivyo, mtu asiyeelewa hii anaweza kuona Mkristo akila. Wanaweza kisha kuhimizwa kula nyama kama kitendo cha ibada kwa sanamu.

<< | >>

1 Corinthians 8:1

Sentensi Unganishi

Paulo anawakumbusha waumini kuwa ingawa sanamu hazina nguvu, waumini lazima wawe makini wasiwaathiri waumini dhaifu wanaoweza kufikiri wanatumikia sanamu. Paulo anawaambia waumini wawe makini katika uhuru walinao kwa Kristo.

Maelezo ya Jumla

"Sisi" inamaanisha Paulo pamoja na waumini wengine.

Sasa kuhusu

Paulo anatumia maneno haya kwenda kwenye sawali lijalo alilokuwa ameulizwa na Wakoritho.

vyakula vilivyotolewa sadaka kwa sanamu

Watu wa imani ya kipagani walitoa nafaka, samaki, ndege, au nyama, kwa miungu yao. Kuhani alitoa sehemu ya dhabihu ili kuichoma kwenye madhabahu.Paulo anazungumzia sehemu iliyo baki, ambayo ilipaswa kurudishwa kwa waabudu au kuuzwa katika soko.

Tunajua kuwa "wote tuna maarifa"

Paulo ananukuu maneno ambayo baadhi ya Wakoritho waliyatumia. "Wote tunajua, kama vile ninyi wenyewe mnapenda kusema, kwamba 'wote tuna maarifa.' "

Maarifa huleta majivuno

" Watu wenye ujuzi mwingi hufikiri wao ni bora zaidi kuliko hali yao halisi."

upendo hujenga

"Upendo ndiyo msaada wa kweli kwa watu"

mtu huyo anajulikana na yeye

"Mungu anamjua mtu huyo"

anadhani kwamba anajua jambo fulani

" anaamini anajua kila kitu kuhusu jambo fulani"

mtu huyo anajulikana naye

katika muundo tendaji "Mungu anamjua mtu huyo"

1 Corinthians 8:4

Maelezo ya Jumla

"Sisi" inamaanisha waumini wote

wajua kuwa "sanamu si kitu katika dunia hii," na ya kuwa hakuna Mungu ila mmoja tu

Paulo ananukuu maneno haya ambayo baadhi ya Wakorintho waliyatumia. "Sote tunajua, kama ninyi wenyewe mnavyopenda kusema, kuwa sanamu haina nguvu au maana kwetu' na kwamba hakuna Mungu ila mmoja tu"'

sanamu katika dunia hii si kitu

"sanamu haina nguvu katika dunia hii"

waitwao miungu

waitwao miungu..." vitu ambavyo watu huviita miungu"

miungu na mabwana wengi.

Paulo hana imani kuwa miungu na mabwana wengi wapo na wanaishi, lakini anatambua kuwa wapagani wao wanaamini hivyo.

ijapokuwa kwetu kuna

" Vyovyote watakavyosema na kufikiri watu wengine , sisi tunaamini kwamba kuna... tunaishi"

1 Corinthians 8:7

Maelezo ya Jumla

Paulo anazungumza kuhusu ndugu walio "dhaifu" watu ambao hawawezi kutofautisha kati ya vyakula vilivyotolewa kwa miungu na ibada ya sanamu. Kama mkristo anakula vyakula vilivyotolewa sadaka kwa miungu, ndugu walio dhaifu wanaweza kufikiri kwamba Mungu amewaruhusu kuabudu miungu kwa kula vyakula vilivyotolewa sadaka kwa miungu hao. Hata kama mlaji hakuabudu miungu bali amekula chakula tu, ataharibu dhamiri ya ndugu yake.

kila mmoja... baadhi

"watu wote...baadhi ya watu miongoni mwa wakristo"

kupotoshwa

"kuharibiwa" au "dhuriwa"

1 Corinthians 8:8

chakula hakitatuthibitisha sisi kwa Mungu

"chakula hakitupi sisi kibali kwa Mungu" au "chakula tunacho kula hakimfanyi Mungu kupendezwa nasi"

Sisi sio wabaya sana kama tusipokula, au wema sana kama tukila

"Baadhi ya watu wanaweza kufikiria kuwa kama hatuli baadhi ya vitu, Mungu atatupenda kidogo. Lakini hawako sahihi. Wale wanao fikiri kuwa Mungu atatupenda zaidi ikiwa tunakula vitu hivyo pia hawako sahihi."

mtu ambaye ni dhaifu

waumini wasio imara katika imani zao

mtu amekuona, wewe uliye

Paulo anaongea kwa Wakorintho kama anaongea na mtu mmoja

Dhamiri yake

mawazo yanayomfanya mtu ajue kati ya jambo zuri na baya.

haitathibitika

" tiwa moyo kula "

1 Corinthians 8:11

ufahamu wako

Paulo anatumia neno "wako" kuongea na Wakorintho wote

aliye dhaifu... anaangamizwa

Kaka au dada asiyekuwa imara katika imani yake atatenda dhambi au kupoteza imani yake.

Kwa hiyo

"kwa sababu nilichoeleza ni kweli"

ikiwa chakula kinasababisha

" chakula" ni picha ya mtu anayekula hicho chakula " kwa kula kwangu kama nitasababisha" au " Ikiwa ninakula na kusababisha"

1 Corinthians 9

1 Wakorintho 09 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Paulo anajitetea katika sura hii. Watu wengine walidai kwamba alikuwa anajaribu kupata fedha kutoka kanisani.

Dhana maalum katika sura hii

Kupata pesa kutoka kanisani

Watu walimshtaki Paulo kwa kutaka fedha tu kutoka kanisani. Paulo alijibu kwamba angeweza kupata fedha kutoka kanisa kwa njia ya haki. Agano la Kale lilifundisha kwamba wale waliofanya kazi wanapaswa kukilisha kutoka kwa kazi zao. Yeye na Barnaba hawakutumia kamwe haki hii kimakusudi ili kujikimu maisha yao wenyewe.

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Mifano

Paulo anatumia mifano nyingi katika sura hii. Sitiari hizi hifundisho maneno ya ukweli ngumu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Muktadha

Kifungu hiki ni muhimu kwa sababu Paulo "anaweka katika muktadha" kuhubiri kwa injili kwa watu mbalimbali. Hii ina maana kwamba Paulo hujiweka mwenyewe pamoja na Injili kueleweka, bila matendo yake kuzuia injili. Mtafsiri anapaswa kuchukua huduma ya ziada kuhifadhi nyanja za "kuwekwa katika muktadha" hii ikiwa inawezekana. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#goodnews)

Maswali ya uhuishaji

Paulo anatumia maswali mengi ya uhuishaji katika sura hii. Anayatumia kusisitiza maneno mbalimbali anapofundisha Wakorintho.(See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-rquestion)

<< | >>

1 Corinthians 9:1

Sentensi Unganisha

Paulo anaelezea anavyotumia uhuru wake katika Kristo

mimi si huru?

Paulo anatumia swali kuwakumbusha Wakorintho juu ya haki alizo nazo. " mimi ni mtu niliye huru."

Mimi si mtume?

Paulo anatumia swali hili kuwakumbusha Wakoritho juu ya vile alivyo na haki aliyo nayo. "Mimi ni mtume."

Mimi sikumwona Yesu Bwana wetu?

Paulo anatumia swali hili kuwakumbusha Wakoritho juu ya vile alivyo. "Nimemuona Yesu Bwana wetu."

Ninyi si matunda ya Kazi yangu katika Bwana?

Paulo anatumia swali hili kuwakumbusha Wakoritho juu ya uhusiano wao kwakwe. "Imani yenu katika Kristo ni matokeo ya kazi yangu katika Bwana."

ninyi ni uthibitisho wa utume wangu katika Bwana.

" ninyi ni kielelzo ambao naweza kutumia kuthibitisha kuwa Bwana amenichagua kuwa mtume "

1 Corinthians 9:3

Huu ndio utetezi wangu

Hapa inaweza kumaanisha 1) maneno yanayofuata ni maneno ya kujitetea kwa Paaulo au 2) maneno katika 9: 1 ni utetezi wa Paulo, " huu ndio utetezi... wangu ninafanya"

Je hatuna haki ya kula na kunywa?

"Tuna haki kabisa kupokea chakula na kinywaji kutoka makanisani."

Hatuna haki ya kuchukua mke aliye amini, kama wafanyavyo mitume wengine, na ndugu wa Bwana, na Kefa?

"Kama tuna wake walioamini, tuna haki ya kuwachukua pamoja nasi kama vile mitume wengine wanavyo wachukua wake zao, na ndugu katika Bwana, na kefa."

Au ni mimi peke yangu na Barnaba ambao tunapaswa kufanya kazi?

Paulo anawatia aibu Wakorintho " Mnafikiri ya kwamba Barnaba na mimi ndiyo watu pekee tunaofanya kazi ili tupate pesa."

1 Corinthians 9:7

Ni nani afanyaye kazi kama askari kwa gharama zake mwenyewe?

" Wote tunajua kuwa askari hatumii vifaa vyake mwenyewe." au " Wote tunajua kuwa kila askari hupokea vifaa kutoka serikalini"

Ni nani apandaye mzabibu asile matunda yake?

" Wote tunajua kuwa yule anayepanda shamba la zabibu atakula matunda yake." au " Wote tunajua kuwa hakuna anayetarajia mtu aliyepanda shamba la zabibu asile matunda yake."

Au na nani achungaye kundi asiyekunywa maziwa yake?

" Wote tunafahamu kuwa wale wachungao kundi hupata kinywaji chao kutoka kundini."

Je ninasema haya kwa mamlaka ya kibinadamu?

"Mnafikiri kuwa ninasema mambo haya kwa matakwa ya mamlaka ya kibinadamu."

Sheria nayo pia haisemi haya?

"Mnatenda haya kana kwamba hamjui hivi ndivyo imeandikwa katika sheria."

1 Corinthians 9:9

usimfunge

Musa alizungumza na wana wa Israeli kama anazungumza na mtu mmoja, hivyo amri hii ipo katika umoja.

Ni kweli kwamba hapa Mungu anajali ng'ombe?

"Mnapaswa kujua bila kuambiwa kuwa siyo ng'ombe ambaye Mungu anamjali zaidi."

Je hasemi hayo kwa ajili yetu?

" Badala yake, Mungu alikuwa anasema kuhusu sisi."

kwa ajili yetu

Hapa "yetu" inarejea kwa Paulo na Barnabas.

ni neno kubwa tukivuna vitu vya mwilini kutoka kwenu?

"Mlipaswa kufahamu kabla hata ya kuwaambia kuwa si jambo kubwa kwetu tukipokea msaada wa vitu kutoka kwenu."

1 Corinthians 9:12

Ikiwa wengine walipata... kwenu, Je! Sisi si zaidi?

Neno "sisi" hapa linamwakilisha Paulo na Barnaba " Wengine walifanya...nanyi mlipaswa kufahamu hata bila kuambiwa kwamba tuna haki zaidi"

Ikiwa wengine walipata haki hii

Wote Paulo na Wakorintho wanajua kuwa wengine walipata haki "Kwamba wengine walipata haki hii"

Wengine

wahubiri wengine wa injili

haki hii

haki waliyonayo waumini wa Korintho ya kuwapatia mahitaji yao wale waliohubiri habari njema kwao

kuwa kikwazo kwa

"kuwa mzigo kwa" au "kuzuia kuenea kwa"

Hamjui ya kuwa wote wafanyao kazi hekaluni hupata chakula chao kutoka hekaluni?

"Nataka niwakumbushe kuwa wale wanaohudumu hekaluni wanapata chakula chao kutoka hekaluni"

wapate kuishi kutokana na hiyo injili

Neno Injili hapa ni lugha ya picha kwa 1) watu waliwahubiria injili, " wanapokea chakula chao na vitu vingine wavyohitaji kutoka kwa watu wanaowafundisha habari njema" au 2) matokeo ya kufanya kazi ya kueneza injili, "wanapokea chakula chao na mahitaji yao mengine kwa sababu wanafanya kazi ya kueneza habari njema"

1 Corinthians 9:15

haki hizi

"vitu hivi ambavyo wanastahili"

ili jambo lolote lifanyike kwa ajili yangu

Katika muundo wa kitenzi tendaji:- "kwa hiyo mtafanya jambo kwa ajili yangu"

kubatilisha huku kujisifu

"kuondo hii fursa ambayo najisifia"

lazima nifanye hivi

"Lazima nihubiri injli"

ole wangu

"itakuwa bahati mbaya"

1 Corinthians 9:17

kama ninafanya hivi kwa hiari

"kama nitahubiri kwa hiari"

kwa hiari

"kwa furaha" au "kwa sababu ninataka"

Bado nina jukumu nililopewa kuwa wakili

katika muundo wa kitenzi tendaji:- "Lazima nifanye kazi hii ambayo Mungu alinip ili kuikamilisha"

thawabu yangu ni nini?

" Hii ndiyo thawabu yangu."

kwamba nihubiripo, niweze kutoa injili bila malipo

"Thawabu yangu kwa ajili ya kuhubiri ni kuwa nihubiri bila kupokea malipo"

kutoa injili

"kuhubiri injili"

na hivyo situmii haki yangu yote ya injili

"kwa hiyo siwaombi watu kunisaidia ninaposafiri na kuhubiri"

1 Corinthians 9:19

kupata zaidi

"kuwashawishi wengine waamini" au "kuwasaidia wengine kuamini katika Kristo"

nilikuwa kama Myahudi

"nilitenda kama Muyahudi" au "niliishi kulingana kwa tamaduni za Kiyahudi"

nilikuwa kama mmoja wao aliye chini ya sheria

"Nilikuwa kama mmoja niliye jidhatiti kufuata matakwa ya uongozi wa Wayahudi, nikikubali uelewa wao wa maandiko ya Kiyahudi"

1 Corinthians 9:21

nje ya sheria

" watu wasiotii sheria ya Musa"

1 Corinthians 9:24

Sentensi Unganishi

Paulo anaeleza kuwa anatumia uhuru wake kujirudi mwenye.

Mnajui ya kuwa katika mbio wote washindanao hupiga mbio, lakini apokeaye tuzo ni mmoja?

Paulo anawakumbusha Wakorintho kwa kitu ambacho wanakijua ili awapashe habari nyingine mpya. " niwakumbushe kuwa ingawa wakimbiaji wote hushiriki katika mbio ni mkimbiaji mmoja tu anayepokea zaidi"

kimbia mbio

Paulo anafananisha kuishi maisha ya Kikristo na kufanya kazi kwa ajili ya Mungu kukimbia mbio na kuwa mwanamichezo. Kama ilivyo katika mbio, maisha ya Kikristo na kazi zinahitaji nidhamu kwenye sehemu ya mkimbiaji, na kama kwenye mashindano Mkristo analo lengo mahususi.

kimbia kupata tuzo

Paulo anaongea habari za tuzo ambazo Mungu huwapa watu wake waaminifu kana kwamba ni ni wakimbiaji wanaoshindana.

taji iharibikayo...taji isiyoharibika.

Taji ni kitita cha maua yaliyosukwa pamoja. Mataji yalitolewa kama zawadi kwa wakimbiaji walioshinda michezo na mashindano. Paulo anaongelea maisha ya milele kama taji isiyonyauka.

mimi sikimbii bila sababu au napigana ngumi kama kupiga hewa

"najua vizuri kwa nini ninakimbia, na ninajua ninachofanya ninapopigana ngumi"

mimi mwenyewe nisiwe wa kukataliwa

" hakimu atasema kwamba nilitii taratibu."

1 Corinthians 10

1 Wakorintho 10 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Sura za 8-10 pamoja zinajibu swali: "Je, inakubalika kula nyama ambayo imetolewa dhabihu kwa sanamu?"

Katika sura hii, Paulo anatumia kutoka kuwaonya watu kutotenda dhambi. Kisha, anarudi kujadili nyama inayotolewa kwa sanamu. Anatumia Mlo wa Bwana kama mfano. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

Dhana maalum katika sura hii

Kutoka

Paulo anatumia uzoefu wa Israeli kutoka Misri na kutembea jangwani kama onyo kwa waumini. Ingawa Waisraeli walimfuata Musa, wote walikufa njiani. Hakuna hata mmoja aliyefikia Nchi ya Ahadi. Wengine waliabudu sanamu, wengine walimjaribu Mungu, na wengine walinung'unika. Paulo anawaonya Wakristo wasitende dhambi. Tunaweza kushinda majaribu kwa sababu Mungu hutoa njia ya kuepuka. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#promisedland)

Kula nyama iliyotolewa dhabihu kwa sanamu

Paulo anazungumzia nyama iliyotolewa kwa sanamu. Wakristo wanaruhusiwa kula, lakini inaweza kuumiza wengine. Kwa hiyo wakati wa kununua nyama au kukula na rafiki, usiulize ikiwa imetolewa kwa sanamu. Lakini ikiwa mtu anakuambia kuwa imetolewa kwa sanamu, usiile kwa ajili ya mtu huyo. Usimkosee mtu yeyote. Jaribu kuwaokoa badala yake. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#save)

Maswali ya uhuishaji

Paulo anatumia maswali mengi ya uhuishaji katika sura hii. Anayatumia kusisitiza maneno mmbalimbali anapofundisha Wakorintho.(See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-rquestion)

<< | >>

1 Corinthians 10:1

sentensi Unganishi

Paulo anawakumbusha Wakorintho mfano wa tabia ambaya( uovu) na ibada ya sanamu wa baba zao wakongwe wa Kiyahudi

baba zetu

Paulo anarejea kwenye wakati wa Musa katika kitabu cha Kutoka wakati Waisraeli walikimbia kupitia bahari ya chumvi wakati majeshi ya Wamisri yakiwafuatilia. Neno "yetu" linamhusu Paulo mwenyewe pamoja na Wakorintho.

walipita katika bahari

Hii bahari inajulikana kwa majina mawili, Bahari ya chumvi na Bahari ya matete.

walipita

"walipita kwa kutembea" au "walisafiri kupitia"

Wote walibatizwa wawe wa Musa katika wingu

"Wote walimfuata na walijidhatiti kwa Musa"

ndani ya wingu

kwa wingu lililowakilisha uwepo wa Mungu na liliwaongoza Waisraeli wakati wa mchana."mwamba" unawakilisha uimara haswa wa Kristo, ambaye alikuwa pamoja nao wakati wote. Wangetegemea ulinzi na faraja yake.

walikunywa kinywaji kile kile cha roho... mwamba wa roho

" walikunywa maji yale yale ambayo Mungu aliyatoa kwenye mwamba kwa muujiza .... mwamba wa rohoni( mwujiza)

mwamba ule ulikuwa ni Kristo

"mwamba" ulikuwa mwamba wa kawaida ulioonekana kwa macho, hata hivi mwamba huo ulikuwa ukiwakilisha nguvu za Kristo zilizofanya kazi ndani yake " alikuwa Kristo aliyefanya kazi kupitia ule mwamba"

1 Corinthians 10:5

hakupendezwa sana

"kutofurahishwa" au "hasirishwa"

wengi wao

" Mababa wa waisraeli"

maiti zao zilisambazwa

"Mungu alitawanya maiti katika eneo lile" au "Mungu aliwaua na kutawanya maiti za miili yao"

jangwani

eneo la jangwa kati ya Misri na Israeli wakopitia Wisraeli katika safari yao ya miaka 40

1 Corinthians 10:7

waabudu sanamu

"watu wanaoabudu sanamu"

walikaa chini kula na kunywa

" walikaa chini kula chakula"

kucheza

Paulo nukuu maandiko ya kiyahudi. Hapa anataka wasomaji wake wafamu kuwa watu walikuwa wakiabudu miungu (sanamu) kwa kuimba, kucheza na kufanya zinaa. Hii haikuwa sherehe ya kawaida

Wakafa siku moja watu ishirini na tatu elfu

"Mungu aliwaua watu 23,000 kwa siku moja"

kwa sababu hiyo

" kwa sababu walitenda matendo mabaya ya zinaa"

1 Corinthians 10:9

walivyofanya na wakaharibiwa kwa nyoka

Hii inaweza kuelezewa katika muundo tendaji: "matokeo yake, waliangazwa na nyoka"

msinung'unike

kulalamika

kuharibiwa na malaika wa mauti

Hii inaweza kuelezewa katika muundo tendaji: " matokeo yake, malaika wa mauti aliwaharibu"

1 Corinthians 10:11

mambo haya yalitokea kwao

"Mungu aliwaadhibu babu zetu"

mifano kwetu.

Hapa "sisi" ina rejea kwa waumini wote.

Yaliandikwa ili yawe mafundisho kwetu

katika muundo tendaji:- " Mungu alitaka Musa ayaandike ili tujifunze kutenda kwa usahihi"

nyakati za mwisho

" siku za mwisho"

asije akaanguka

hafanyi dhambi au kumkana Mungu

Hakuna jaribu lililowapata ninyi lisilo kawaida ya wanadamu

katika mtazamo chanya "majaribu ambayo yanawaathiri ninyi ni majaribu ambayo yanawapata watu wote."

Hatawaacha mjaribiwe kupita uwezo wenu

" Mungu ataruhusu mjaribiwe katika namna ambayo mtakuwa imara kiasi cha kutosha kupata ushindi"

Hatawaacha mjaribiwe

maelezo katika muundo tendaji "hataruhusu mtu yeyote awajaribu"

1 Corinthians 10:14

Sentensi Unganishi

Paulo anaendelea kuwakumbusha Wakorintho kuwa wasafi na kujitenga ibada ya sanamu na uchafu, wanapokuwa katika ushirika ambao unawakilisha damu na mwili wa Kristo.

ikimbieni ibada ya sanamu

Paulo anazungumzia tendo la kuabudu sanamu ni kama mnyama hatari " fanyeni kila namna ili kukaa mbali na ibada ya kuabudu sanamu"

kikombe cha baraka

Paulo anatumia maelezo haya kufafanua kikombe kilichowekewa divai ambayo ilitumiwa katika meza ya Bwana.

Mkate ule tuumegao, si ushirika wa mwili wa Kristo?

" tunamshukuru Mungu kwa ajili ya kikombe"

si ushirika wa damu ya Kristo?

Kikombe cha divai ambacho tunashiriki kinatuunganisha kushiriki katika damu ya Kristo. kwa maneno mengine "tunashiriki katika damu ya Kristo."

Mkate ule tuumegao, si ushirika wa mwili wa Kristo?

" tunashiriki katika mwili wa Kristo tunaposhiriki mkate"

ushirika wa

"kushiriki katika" au " kushiriki katika hali ya usawa pamoja na wengine"

mkate mmoja

kipande kimoja cha mkate uliookwa na kugawanywa au kukatwa katika vipande vidogo vidogo kabla ya kuliwa.

1 Corinthians 10:18

Wale wote walao dhabihu si washiriki katika madhabahu?

Paulo anawakumbusha Wakorintho jambo wanalolifahamu ili baada ya hapo awape habari mpya. kwa maneno mengine anasema " wale wanaokula sadaka wanashiriki katika shughuli na baraka za madhabahu"

Nasema nini basi?

Paulo anawakumbusha Wakorintho jambo wanalolifahamu ili baada ya hapo awape habari mpya:- " kwa kufanya marudio ya kile nilichosema" au " Hiki ndicho ninacho maanisha"

kuwa sanamu ni kitu?

"Tambueni ninachosema kuwa sanamu siyo kitu halisi"

Au ya kuwa chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu ni kitu?

" Mnafahamu sisemi chakula kilichotelewa sadaka kwa sanamu si kitu muhimu"

1 Corinthians 10:20

Hamwezi kunywea kikombe cha Bwana na kikombe cha mapepo

Paulo anazungumzia habari ya mtu anayenywea kikombe kile kile ambacho mapepo hunywea kuonyesha kuwa mtu huyo ni rafiki wa mapepo. kwa maneno mengine " haiwezekani kuwa rafiki wa kweli kwa wote, Bwana na mapepo"

Hamuwezi kuwa na ushirika katika meza ya Bwana na katika meza ya mapepo

" Haiwezekani kuwa na urafiki wa kweli kwa watu wa Mungu na mapepo pia"

Au twamtia Bwana wivu?

Paulo anataka Wakorintho kujibu swali hili katika mioyo yao " Mnapaswa kujua hata kabla ya kuwaambi ya kuwa haifai kumtia wivu Bwana"

twamtia

kukasirika au kukera

Tuna nguvu zaidi yake?

Paulo anataka Wakorintho kujibu swali hili katika mioyo yao " Mnapaswa kujua hata kabla ya kuwaambi ya kuwa hatuna nguvu kuliko Mungu"

1 Corinthians 10:23

Sentensi Unganishi

Paulo anawakumbusha tena kuhusu sheria ya uhuru na kufanya kila kitu kwa faida ya wengine

Vitu vyote ni halali,

Hapa inaweza kumaanisha 1) Paulo pengine anatoa majibu kutokan na mawazo wanayofikiria Wakorintho " wengine wanasema, 'Naweza kufanya jambo lolote'" au 2) Paulo anasema kile anachodhani ni kweli, " Mungu ameniruhusu nifanye kila kitu."

viwajengavyo watu.

"wasaidie watu"

1 Corinthians 10:25

pasipo kuuliza maswali ya dhamiri.

" Mungu anataka ule chakula kwa dhamiri njema"

1 Corinthians 10:28

Lakini mtu... dhamiri ya yule mwingine

hapa inaweza kumaanisha " kuleni chochote kinawekwa mbele yenu bila kuuliza maswali yanayotokana na dhamira"

Lakini mtu akiwaambia,....msile. Hii ni kwa ajili yake aliyewaambia...ajili ya dhamiri.

Paulo anawaambia Wakorintho "usilile",kana kwamba anaongea na mtu mmoja.Lakini Paulo anatumia umoja kuwapa maelekezo waumini wote wa Korintho.

Maana kwanini...dhamiri? Ikiwa mimi natumia... nimeshukuru kwacho?

Maana zinazowezekana ni 1)" siulizi maswali juu ya dhamiri , je kwanini.. dhamiri? kama nashiriki ... kutoa shukrani?" au 2) Paulo ananukuu kila ambacho Wakorintho walikuwa wakifikiria " baadhi watakuwa wanafikiri , kwa nini ... dhamiri? ikiwa.. nashukuru?"

Maana kwanini uhuru wangu uhukumiwe na dhamiri ya mtu mwingine?

msemaji anataka msikilizaji wake ajibu swali katika akili yake " kabla ya kukuambia ulipaswa kufahamu kuwa hakuna mtu anayeweza kusema nafanya jambo baya kwa kuwa anatumia mawazo yake wala si mawazo yangu, kuhukumu baya na zuri, japo mazo yake ni tofauti na ya kwangu"

Ikiwa mimi natumia chakula kwa shukrani, kwanini nitukanwe kwa kitu ambacho nimeshukuru kwacho?

msemaji anataka msikilizaji wake ajibu swali katika akili yake " nashiriki mlo kwa shukurani, hivyo hakuna mtu anayeweza kunishutumu kwa kile ambacho nakitolea shukurani"

natumia

Neno "mimi" linawakilisha wale ambao wanakula nyama kwa shukurani. " ikiwa mtu atashiriki" au "wakati mtu anapokula"

shukrani

" na shukuru Mungu kwa hicho"au " na mshukuru mtu anayenipatia hicho"

1 Corinthians 10:31

Msiwakoseshe Wayahudi au Wayunani

"Msiwachukize Wayahudi au Wayunani" au "Msiwafanye Wayahudi na Wayunani kukasirika"

kuwapendeza watu wote

"wafanye watu wote wafurahi"

Sitafuti faida yangu mwenyewe

"Sifanyi mambo ninayotamani mimi binafsi"

wengi

watu wengi kadri iwezekanavyo.

1 Corinthians 11

1 Wakorintho 11 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Huu ni mwanzo wa sehemu mpya wa barua (Sura za 11-14). Paulo sasa anazungumza kuhusu huduma nzuri za kanisa. Katika sura hii, anahusisha matatizo mawili tofauti: wanawake katika huduma za kanisa (mistari ya 1-16) na Meza ya Bwana (mistari ya 17-34).

Dhana maalum katika sura hii

Mazoezi mema katika huduma ya kanisa

Wanawake wasio na adabu

Maagizo ya Paulo hapa yanajadiliwa na wasomi. Labda kulikuwa wanawake ambao walikuwa wakitumia uhuru wao wa Kikristo vibaya a kuleta fujo ndani ya kanisa sababu hawakukuwa na adabu ya kawaida. Fujo kutokana na vitendo vyao vilimfanya awe na wasiwasi.

Meza ya Bwana

Kulikuwa na matatizo katika Wakorintho kwa jinsi walikula Meza ya Bwana. Hawakutenda kwa umoja. katika Wakorintho kwa jinsi walikula Meza ya Bwana, baadhi yao walikula chakula chao wenyewe bila kushirikiana. Baadhi yao walilewa wakati watu masikini walipokuwa na njaa. Paulo alifundisha kwamba waumini wanadharau kifo cha Kristo kama wanakula Meza ya Bwana na kufanya dhambi au wakati wanavunja ushirika na wenzao. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#reconcile)

Mifanyo ya muhimu za matamshi katika sura hii

Maswali ya uhuishaji

Paulo hutumia maswali ya uhuishaji ili kuwakaripia watu kwa kutofuata kwao sheria za ibada aliyopendekeza. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-rquestion)

Kichwa

Paulo anatumia "kichwa" kama kielelezo cha mamlaka katika mstari wa 3 na pia kutaja kichwa halisi cha mtu katika mstari wa 4 na kuendelea. Kwa kuwa hayo ni ya karibu sana, inawezekana kwamba Paulo alitumia "kichwa" kwa makusudi kwa njia hii. Hii inaonyesha kwamba mawazo katika aya hizi ziliunganishwa. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metonymy)

<< | >>

1 Corinthians 11:1

Sentensi Unganisha

Baada ya Paulo kuwakumbusha Wakorintho kumfuata yeye kama navyomfuata Kristo, Paulo anatoa maagizo mahususi jinsi wanawake na wanaume wanavyopaswa kuishi kama waumini

"fikiri juu ya" au " kumbuka"

nataka

inaweza kumaanisha 1) "Kwa sababu ya hili, ninataka" au 2) "Hata hivyo, ninataka."

ni kichwa cha

anamamlaka juu ya

naye mwanaume ni kichwa cha mwanamke

inaweza kumaanisha 1) " wanaume wanamamlaka kwa wanawake" au 2) mume anapaswa kuwa na mamlaka kwa mke"

akiwa amefunika kichwa

" anapofunika au kuweke kitambaa kwenye kichwa chake"

anakiabisha kichwa chake

inaweza kumaanisha 1) " hujitia aibu mwenyewe" au 2) huleta aibu kwa Krito, ambaye ni kichwa cha mwanaume."

1 Corinthians 11:5

mwanamke aombae...anakiaibisha kichwa chake

Hii inaweza kumaanisha 1) "wanamke anayeomba ...hujiaibisha mwenyewe" au 2) mke anayeomba...huleta aibu kwa mume wake"

kichwa chake kikiwa wazi

bila vazi lililovaliwa juu ya kichwa ambalo lilifunika mabega na nywele

kukata nywele zake

ni kana kwamba ameondoa nywele zake zote kwenye kichwa chake kwa wembe

ni aibu mwanamke

Ilikuwa ni ishara ya aibu au uzalilishaji kwa mwanamke kunyoa nywele zake au kuzipunguza

kufunika kichwa chake

Mwanamke kuvaa nguo ambayo ilivaliwa juu ya kichwa iliyofunika mabega pamoja na nywele.

1 Corinthians 11:7

haimpasi mwanamume kufunika kichwa chake

ikielezwa katika muundo tendaji, inaweza kumaanisha 1) "ni lazima mwanaume asifunike kichwa chake" au 2) " mwanaume hahitaji kufunika kichwa chake"

utukufu wa mwanaume

Kama vile mwanaume anavyobeba taswira ya ukuu wa Mungu, mwanamke huonyesha tabia ya mwanaume.

Maana mwanamume hakutokana na mwanamke. Badala yake, mwanamke alitokana na mwanamume

Mungu alimuumba mwanamke kwa mfupa kutoka kwa mwanaume. kwa maneno mengine " Mungu hakumuumba mwanaume kutoka kwa mwanamke . Badala yake Mungu alimuumba mwanamke kutoka kwa mwanaume"

1 Corinthians 11:9

Wala...kwa mwanaume

Maneno haya yanarejea katika 11:7 kumaanisha kuwa " mwanamke ni utukufu wa mwanaume"Maana zinazo wezekana ni 1) "kuonyesha mfano kuwa anaye mwanamume kama kichwa chake" au 2) "kuonyesha mfano kuwa anamamlaka ya kuomba na kutoa unabii."

kuwa na ishara ya mamlaka juu ya kichwa chake,

Hapa inaweza kumaanisha 1) "kuonyesha mfano kuwa anaye mwanamume kama kichwa chake" au 2) "kuonyesha mfano kuwa anamamlaka ya kuomba na kutoa unabii"

1 Corinthians 11:11

Hata hivyo

" Pamoja na kwamba nilichosema ni kweli, swala la muhimu ni hili:"

katika Bwana

Hapa inaweza kumaanisha 1) "kati ya Wakristo, ambao ni wa Bwana" au "katika dunia kama ilivyoumbwa na Mungu."

mwanamke hayupo peke yake pasipo mwanamume, au mwanamume pasipo mwanamke.

Hii inaweza kuelezwa katika mtazamo chanya:- " mwanamke anamtegemea mwanaume, na mwanaume anamtegemea mwanamke"

vitu vyote hutoka kwa Mungu.

" Mungu aliumba kila kitu"

1 Corinthians 11:13

Hukumuni wenyewe

"Hukumuni suala hili kulingana na desturi za ndani na taratibu za kanisa mnazozijua"

Ni sahihi mwanamke amwombe Mungu hali kichwa chake kikiwa wazi?

Ikielezewa katika muundo tendaji:-"Kwa kumheshimu Mungu, mwanamke lazima amwombe Mungu akiwa amefunika kichwa chake."

Je hata asili peke yake haiwafundishi...kwake?

Paulo anatarajia Wakorintho wakubaliane naye kuwa " Hali ya asili huwafundisha" kwa maneno mengine " Mnajua hili kwa kutazama watu wanavyofanya kila mara"

amepewa zile nywele

" Mungu alimuumba mwanamke na nywele"

1 Corinthians 11:17

Sentensi Unganishi

Paulo anapozungumzia ushirika mtakatifu, nawakumbusha kuwa na umoja na tabia njema. Anawakumbusha kuwa wakikosa umoja na tabia njema wakati wa ushirika wataugua na kufa, kama ambayo imekwisha tokea kwa baadhi yao.

atika maagizo yafuatayo, mimi siwasifu

Hapa inaweza kumaanisha "ninapotoa maelekezo haya, kunajambo ambalo siwezi kuwasifia"

maagizo

" maelekezo" au "taratibu (sera)"

mnapokusanyika

" kusanyika pamoja"

sio kwa faida bali kwa hasara

" hamsaidiani badala yake mnaumizana"

kanisani

Paulo hazungumzii kuingia ndani ya jengo bali anazungumzia "waumini"

kuna migawanyiko kati yenu

" mnagawanyika wenyewe katika makundi"

ili kwamba wale waliokubaliwa wajulikane kwenu.

Maana zinazokubalika 1) "ili kwamba watu wajue waumini wanao heshimiwa zaidi kati yenu" au 2) "ili kwamba watu waonyeshe kuwakubali waumini fulani kati yenu."

wale waliokubaliwa

Hapa inaweza kumaanisha1) "walinakubaliwa na Mungu" au 2) " ambao kanisa linawakubali"

1 Corinthians 11:20

mkutanikapo

"kusanyika pamoja"

mnachokula sio chakula cha Bwana.

" mnaaminia kuwa mnakula chakula cha Bwana lakini hamukiheshimu kama inavyostahili"

za kulia na kunywea

"ambapo mnaweza kukutana kula chakula"

mnalidharau

chukia au tendea bila adabu na heshima

kuwafedhehesha

aibisha au sababisha kujisikia aibu

Niseme nini kwenu? Niwasifu?

Paulo anawakemea Wakorintho. Kwa maneno mengine anasema " siwezi kusema neno lolote zuri juu ya hili. Siwezi kuwasifu"

1 Corinthians 11:23

Kwa maana nilipokea kutoka kwa Bwana kile ambacho nimewapa ninyi ya kuwa Bwana

" kwa kuwa nilichosikia kutoka kwa Bwana ndicho niliwaambia ninyi, na ilikuwa hivi: Bwana"

usiku ule aliposalitiwa

kielezwa kwa muundo tenda: "usiku ule Yesu aliposalitiwa na Yuda Iskariote "

aliuvunja

" aliupasua mkate katika vipande vidogo vidogo"

Huu ndio mwili wangu

"Mkate ninaoshikilia ni mwili wangu"

1 Corinthians 11:25

kikombe

Hapa inaweza kumaanisha 1) kikombe cha divai ambacho ambacho kilitegemewa akitumie 2) kikombe cha tatu au cha nne miongoni mwa vikombe vinne ambavyo Wayahudi walitumia kunywa divai wakati wa mlo wa Pasaka.

Fanyeni hivi mara nyingi kila mywapo

"Kunyweni kutoka katika kikombe hiki, na kila mara mnapokunywa kitumieni"

mwaitangaza mauti ya Bwana

fundisheni kuhusu kusulubishwa na ufufuo

mpaka atakapokuja

Yesu atakaporudi itasemwa wazi. Kwa maneno mengine " mpaka Yesu atakaporudi tena duniani"

1 Corinthians 11:27

kula mkate na kuywa kikombe cha Bwana

" kula mkate wa Bwana au kunywa kikombe cha Bwana"

chunguza

Paulo aneleza uhusiano wa mtu na Mungu, jinsi mtu anavyoishi katika maisha yake kwamba anatakiwa ayaangalie maisha yake na kuyatathmini kama mtu ayetaza kitu anapotaka kukinunua.

bila kuupambanua mwili

Inaweza kumaanisha1) "na hatambui kuwa kanisa ni mwili wa Bwana" au 2) "na hafikiri kuwa anashiriki mwili wa Bwana."

wagonjwa na dhaifu

Maneno haya yanamaana zizokaribiana: kuwa nyonge, kuwa na madhara

1 Corinthians 11:31

tunajichunguza

Paulo aneleza uhusiano wa mtu na Mungu, jinsi mtu anavyoishi katika maisha yake kwamba anatakiwa ayaangalie maisha yake na kuyatathmini kama mtu ayetaza kitu anapotaka kukinunua.

hatutahukumiwa

ikielezwa kwa muundo tendaji:" Mungu hatatuhukumu"

tunapohukumiwa na Bwana, twarudiwa, ili tusije tukahukumiwa

ikielezwa kwa muundo tendaji:" Mungu anatuhukumu, anatusahihisha, ili asije akatushutumu"

1 Corinthians 11:33

mkutanikapo mpate kula

kusanyikeni kula chakula pamoja kabla ya kusherekea chakula cha Bwana

ngojeaneni

" Kabla ya kuanza kula wasubirie na wengine hadi wafike"

ale nyumbani kwake

"ale kabla ya kuhudhuria mkutano huu"

isiwe kwa hukumu

" lisiwe tukio la Mungu kuwaadhibu"

1 Corinthians 12

1 Wakorintho 12 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Vipaji vya Roho Mtakatifu

Sura hii inaanza sehemu mpya. Sura za 12-14 zinajadili vipaji vya kiroho ndani ya kanisa.

Dhana maalum katika sura hii

Kanisa, mwili wa Kristo

Hii ni mfano muhimu katika Maandiko. Kanisa lina sehemu nyingi. Kila sehemu ina kazi tofauti. Zinakusanywa kuunda kanisa moja. Sehemu zote tofauti ni muhimu. Kila sehemu inapaswa kujali sehemu nyingine zote, hata zile zinazoonekana kutokuwa muhimu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Hakuna mtu anayeweza kusema, 'Yesu ni Bwana,' isipokuwa kwa Roho Mtakatifu."

Katika kusoma Agano la Kale, Wayahudi wangeweza kubadilisha neno "Bwana" kwa neno "Yahweh." Sentensi hii ina maana kwamba hakuna mtu anayeweza kusema kuwa Yesu ndiye Bwana, Mungu katika mwili, bila uwezo wa Roho Mtakatifu kuwavuta kukubali ukweli huu. Ikiwa neno hili limetafsiriwa vibaya, linaweza kuwa na madhara ya kitheolojia yasiyotarajiwa.

<< | >>

1 Corinthians 12:1

Sentensi Uganishi

Paulo anawafahamisha kuwa Mungu ametoa karama maalumu kwa waumini. Karama hizi ni kwa ajili ya kuusaidia mwili wa waumini.

Sitaki mkose kufahamu

"Ninataka mfahamu"

mlipotoshwa kufuata sanamu zisizoongea

ikielezwa kwa muundo tendaji: "mliamini uongo na mlibudu sanamu zisizoongea"

kwa njia zozote mliongozwa nazo

ikielezwa kwa muundo tendaji:" na ziliwaongoza kwa namna nyingi"

hakuna yeyote anenaye kwa Roho wa Mungu awezaye kusema

maana zinazowezekana ni 1) "hakuna Mkristo ambaye ana Roho wa Mungu ndani yake, awezaye kusema," au 2) "hakuna atoaye unabii kwa nguvu ya Roho wa Mungu awezaye kusema."

Yesu amelaaniwa.

" Mungu atamwadhibu Yesu" au Mungu atamtesa Yesu"

1 Corinthians 12:4

azitendaye kazi zote katika wote

"humwezesha kila mtu kupokea"

1 Corinthians 12:7

kila mmoja hupewa

Hapa ikielezwa kwa muundo tendaji:- Mungu ndiye anayefanya tendo la upaji au utoaji. kwa maneno mengine "Mungu humpa kila mmoja "

mtu mmoja amepewa na Roho neno

ikielezwa kwa muundo tendaji:- "Kwa njia ya Roho Mungu humpatia kila mmoja neno"

kwa Roho

Mungu hutoa karama kupitia kazi ya Roho

hekima...maarifa

Tofauti kati ya haya maneno mawili siyo muhimu, cha muhimu ni kwamba maarifa na hekima hutoka kwaMungu kwa njia ya Roho yule yule.

neno la hekima

" maneno ya busara"

neno la maarifa

" Maneno yanayoonesha ujuzi"

1 Corinthians 12:9

humpa

Hii inaweza kuelezewa katika muundo tendaji " Mungu hutoa"

kwa Roho mmoja

Mungu hutoa karama kupitia kazi ya Roho Mtakati pekee.

aina mbalimbali za lugha

"uwezo wa kuongea lugha mbalimbali"

tafsiri za lugha

uwezo wa kutoa mafafanuzi ya lugha nyingine inayozungumzwa ambayo si lugha yako.

kufasiri

Hii inamaanisha kufafanua kile anachosema mtu kwa lugha isiyofahamika kwa wengine. au kueleza maana za maneno kutoka lugha moja kwenda lugha nyingine

Roho ni yule

Paulo anawakumbusha wasomaji wake kuwa " Roho ni yule yule... Roho moja"

1 Corinthians 12:12

Sentensi Unganishi

Paulo anaendelea kusema juu ya karama ambazo Mungu amewapa waumini , Mungu ametoa karama mbalimbali kwa waumini tofauti tofauti, lakini pamoja na hilo waumini wamefanywa kuwa mwili mmoja , ambao unaitwa mwili wa Kristo. Kwa sababu hii waumini wanapaswa kuwa na umoja.

katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, kwamba tu Wayahudi au Wa

Hapa inaweza kumaanisha 1) Roho mtakatifu ndiye anayetubatiza, " kwa Roho moja tunabatizwa" or 2) Roho ni kama maji ya ubatizo ni njia iliyotumika kutubatiza kuwa mwili mmoja, " katika Roho moja tulibatizwa"

wote walifanywa kunywa kwa Roho mmoja

"Mungu alitupa sisi sote Roho mmoja, na tunashiriki Roho kama watu wawezavyo kushiriki kinywaji"

wote tulinyweshwa Roho mmoja

Hii inaweza kuelezewa katika muundo wa kitenzi "Mungu ametupatia Roho mmoja, na tunashiriki katika Roho huyo kama watu wanavyo weza kushiriki kinywaji cha aina moja"

1 Corinthians 12:14

kungekuwa wapi kusikia?...kungekuwa wapi kunusa?

Maneno haya ukiyabadili kuwa sentensi: "usingeweza kusikia chochote...usingeweza kunusa chochote"

1 Corinthians 12:18

kiungo kimoja

Kwa ujumla neno "Kiungo" linarejea sehemu zote za mwili kama vile kichwa, mkono au goti. kwa maneno mengine "sehemu ile ile ya mwili"

mwili ungelikuwa wapi?

"kusingelikuwa na mwili"

Kwa hiyo sasa kuna viungo vingi, lakini

kwa maneno mengine ni kusema "kusingekuwa na mwili"

1 Corinthians 12:21

haliwezi kuuambia mkono, "sina haja na wewe."

Neno "wewe" lipo katika hali ya ummoja

onekana kuwa na heshima kidogo

"siyo muhimu sana"

visivyotajwa

Hii pengine inarejea kwenye sehemu za siri za mwili, ambazo huwa vimefunika.

1 Corinthians 12:25

pasiwepo na migawanyiko katika mwili, bali

"mwili uwe na umoja, na"

kiungo kimoja kinaheshimiwa

katika muundo tendaji ni kwmba " mmoja hutoa heshima kwa mwajuiya mwingine"

Sasa ninyi

Neno "Sasa" linatumika kuvuta usikivu kwenye dokezo muhimu linalofuatia

1 Corinthians 12:28

kwanza mitume

Hii inaweza kumaanisha 1) " ninataja karama ya kwanza kuwa ni ya mitume" au 2) "karama ya muhimu zaidi ni ya mitume"

wale wasaidiao

" wale wanaotoa msaada kwa waumini wenzao"

wale wafanyao kazi ya kuongoza

" wale wanaosimamia kanisa"

wote walio na aina mbalimbali za lugha

Watu wanaozungumza lugha za kigeni moja au zaidi bila kujifunza.

Je sisi wote ni mitume? wote ni manabii? wote ni waalimu? wote wanafanya matendo ya miujiza?

Paulo anawakumbusha wasomaji wake jambo wanalolijua. kwa maneno mengine anasema " baadhi yao tu ni mitume. Baadhi yao tu ni manabii. Baadhi yao tu hufanya matendo ya miujiza"

1 Corinthians 12:30

Je wote mnakarama ya uponyaji?

Kwa maneno mengine " si watu wate wanakarama ya uponyaji"

wote mnaongea kwa lugha?

Kwa maneno mengine " si watu wote hunenea kwa lugha"

wote mnatafasiri lugha?

kwa maneno mengine "si wote hufasiri lugha"

Kufasiri

Hii inamaanisha kufafanua kile anachosema mtu kwa lugha isiyofahamika kwa wengine. au kueleza maana za maneno kutoka lugha moja kwenda lugha nyingine

Tafuteni sana karama zilizo kuu

Hapa inaweza kumaanisha 1) "tafuteni kwa bidii Mungu awape karama zinazoweza kulisaidia kanisa vizuri zaidi"

1 Corinthians 13

1 Wakorintho 13 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Paulo anaonekana kuacha mafundisho yake kuhusu vipaji vya kiroho. Hata hivyo, labda sura hii hutumika pakubwa katika mafundisho yake.

Dhana maalum katika sura hii

Upendo

Upendo ni sifa muhimu zaidi ya mwamini. Sura hii inaeleza kikamilifu kuhusu upendo. Paulo anaeleza kwa nini upendo ni muhimu zaidi kuliko vipaji vya Roho. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#love)

mifano mhimu ya matamshi katika sura hii

Mifano

Paulo anatumia mifano nyingi tofauti katika sura hii. Anatumia sitiari hizi kuwafundisha Wakorintho, hasa katika mada ngumu. Wasomaji mara nyingi wanahitaji ufahamu wa kiroho kuelewa mafundisho haya. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

<< | >>

1 Corinthians 13:1

Sentensi Unganishi

Baada ya kuzungumzia karama ambazo Mungu amewapa waumini, Paulo anasisitiza jambo la muhimu zaidi.

lugha...malaika

Hapa inaweza kumaanisha 1) Paulo atumia lugha ya kukuza jambo ili ujumbe wake ueleweke, lakini hamaanishi kwamba wanadamu wanaweza kuongea lugha ambayo malaika hutumia. au 2) Paulo anafikiri kuwa baadhi ya watu ambao hunena kwa lugha huwa wananena lugha inayotumiwa na malaika.

nimekuwa shaba iliayo au upatu uvumao

nimekuwa kama chombo kinachotoa sauti kubwa, sauti inayokera na kusumbua

upatu uvumao

chombo chenye umbo la sinia, kinachofunikwa kwenye kitu kingine na kupigwa ili kutoa sauti.

ninautoa mwili wangu ili nichomwe moto

kwa kutumia kitenzi tendaji ni sawa na kusema "ninawaruhusu watesi wangu wanichome moto hadi kufa"

1 Corinthians 13:4

Upendo huvumilia na hufadhili....huvumilia mambo yote

Paulo anazungumzia upendo kama kitu chenye nafsi hai.

hauoni uchungu haraka,

Hii inaweze kuelezewa katika muundo tendaji kama " hakuna mtu atakayeufanya upendo upate hasira kwa haraka"

Haufurahii udhalimu. Badala yake, hufurahi katika kweli

"hufurahia katika uadilifu na kweli"

1 Corinthians 13:8

Upendo

Kumpenda mtu mwingine ni kumjali na kufanya mambo ambayo yatamletea faida au kumnufaisha. Upendo upo aina mbalimbali 1. Upendo unaotoka kwa Mungu huwa unakusudia kuleta mema kwa wengine, huwa haulengi kujinufaisha kwa mtu mmoja. Mungu mwenyewe ni upendo na chanzo cha upendo.

Nabii, unabii

Nabii ni mtu anayeleta ujumbe kutoka kwa Mungu kwenda kwa watu. Mara nyingi manabii huwaonya watu kutoka katika dhambi ili kumtii Mungu. Unabii ni ujumbe unaotolewa na Nabii

Lugha

Katika Biblia neno Lugha humaanisha, lugha za wanadamu zinazotumiwa na makundi mbalimbali ya watu. Wakati mwingine neno Lugha humaanisha lugha ya kiroho ambayo Roho Mtakatifu huwapa waumini kama moja ya "zawadi au karama za Roho"

kujua, maarifa

kujua ni kuelewa kitu au kufahamu jambo, kutambua. maarifa ni neno linalohusiana na habari ambayo watu wanaifahamu.

Kamili

Katka Biblia neno hili humaanisha kukomaa ua kukua katika maisha ya kiroho. Kufanya kitu kikamilike ni kukifanyia kazi hadi kiwe kizuri bila dosari.

1 Corinthians 13:11

Kwa kuwa sasa tunaona kama kwa kioo

Vioo nyakati alizoishi Paulo vilitengenezwa kwa chuma kilichopakwa rangi hivyo vilionesha taswira yenye giza tofauti na vioo vya glass vya siku hizi

sasa tunaona

Hapa inaweza kumaanisha 1) "sasa tunamwona Kristo" au 2) "sasa tunamwona Mungu"

uso kwa uso

Tutamwona Kristo uso kwa uso. Hapa inamaana kwamba tutakuwa pamoja na Kristo katika hali ya mwili.

nitajua sana

" nitamjua Kristo kwa ukamilifu"

kama na mimi ninavyojulikana sana

katika muundo tendaji inaweza kuelezewa "kama Kristo avyonifahamu kikamilifu"

Lakini sasa mambo haya matatu yanadumu

" Nimuhimu kwamba...sasa"

imani, tumaini lijalo, na upendo

" tunamwamini Kristo, tukijua kwamba atafanya vitu vyote alivyoahidi, tunampenda na tunapendana sisi kwa sisi"

1 Corinthians 14

1 Wakorintho 14 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Katika sura hii, Paulo anaandika tena kuhusu vipaji vya kiroho.

Baadhi ya tafsiri huweka kile kinanukuliwa kutoka kwenye Agano la Kale kwa upande wa kulia zaidi kwenye ukurasa; zaidi ya maandiko yote. ULB inafanya hivyo kwa maneno ya mstari wa 21.

Dhana maalum katika sura hii

Ndimi

Wasomi hawakubaliani juu ya maana halisi ya kipaji cha ndimi. Paulo anaelezea kipaji cha ndimi kama ishara kwa wasioamini. Haitumiki kwa kanisa lote, isipokuwa mtu akielezea kile kinachosemwa. Ni muhimu sana kwamba kanisa linatumia kipaji hiki vizuri.

Unabii

Wasomi hawakubaliani juu ya maana halisi ya unabii kama kipaji cha kiroho. Paulo anasema manabii wanaweza kujenga kanisa lote. Anaelezea unabii kama kipaji kwa waumini. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#prophet)

<< | >>

1 Corinthians 14:1

Sentensi Unganishi

Paulo anataka ifahamike kuwa kufundisha ni muhimu kwa sababu watu wanapata maelekezo kwa njia ya kufundishwa, hivyo kazi ya kufundisha lazima ifanywe kwa upendo.

Utafuteni upendo

" ufuateni upendo" jitahidini kuwapenda watu"

zaidi sana mpate kutoa unabii

" na fanyeni kazi kwa bidii ili muweze kutoa unabii"

kuwajenga

" kuwasaidia watu"

1 Corinthians 14:5

Yeye atoaye unabii ni mkuu

Paulo anasisitiza kuwa karama ya kutoa unabii ni kuu zaidi kuliko karama ya kunena kwa lugha. kwa maneno mengine "Anayetoa unabii karama yake ni kuu zaidi"

tafasiri

Hii inamaanisha kufafanua kile anachosema mtu kwa lugha isiyofahamika kwa wengine. au kueleza maana za maneno kutoka lugha moja kwenda lugha nyingine

nitawafaidia nini ninyi

kwa maneno mengine "Sitawasaidia" au " nitakuwa sijafanya jambo lolote la kuwasaidia"

1 Corinthians 14:7

visipotoa sauti zilizo na tofauti

Hii inareje sauti tofauti tofauti zinazotokana na midundo inayotoa tuni, haimaani tofauti kati ya sauti ya filimbi na kinubi tu.

itatambulikanaje ni chombo gani kinachezwa

Kwa maneno mengine " hakuna mtu atakaye tambua tuni ya filimbi au kinubi kinapogigwa"

1 Corinthians 14:10

hakuna hata moja isiyo na maana

" Zote zina maana"

1 Corinthians 14:12

uthihirisho wa Roho

" muweze kufanya matendo yanadhihilisha kuwa Roho anawaongoza na kuwatawala"

takeni kwamba mzidi sana kulijenga kanisa

" muwe na mafanikio makubwa katika kuwawezesha watu wa Mungu kumtumikia Yeye zaidi"

kutafasiri

Hii inamaanisha kufafanua kile anachosema mtu kwa lugha isiyofahamika kwa wengine. au kueleza maana za maneno kutoka lugha moja mpaka lugha nyingine. Anagalia 2:12 kwa maelezo zaidi kuhusu "tafasiri"

akili zangu hazina matunda

"Siyafamu maneno ninayoyasema"

1 Corinthians 14:15

Nifanye nini?

Paulo anatoa utangulizi wa maamuzi yake. kwa maneno mengine anasema "hivi ndivyo nitakavyofanya"

Nitaomba kwa roho yangu...nitaomba kwa akili zangu. Nitaimba kwa roho yangu...nitaimba kwa akili zangu

Maombi na nyimbo lazima ziwe katika lugha inayoeleweka kwa watu waliopo

kwa akili zangu

" kwa maneno yanayoeleweka kwangu"

ukimsifu Mungu... utoapo shukurani.. usemayo

Paulo anatumia neno "wewe" kutoa ujumbe kwa kila mtu anayeomba katika roho lakini si katika akili yake.

mgeni ataitikaje "Amina"

kwa maneno mengine " Mgeni hataweza kusema Amina"

ataitikaje "Amina"

" kukubali"

1 Corinthians 14:17

wewe washukuru

Paulo anatumia neno "wewe" kuzungumza na Wakorintho wote.

hajengwi

Paulo anasema swala la kuwasaidia watu ni kama kujenga nyumba. lakini bado " mwingine hasaidiki"

maneno kumi elfu

Inamaanisha "maneno elfu kumi au maneno mengi zaidi ya hayo".

1 Corinthians 14:20

Maelezo ya Jumla

Paulo anawaambia kuwa kunena katika lugha mbalimbali kulitabiliwa tangu zamani na nabii Isaya, hii ilikuwa miaka mingi kabla ya tukio la kunena kwa lugha lilotukia siku ya kuanza kwa kanisa la Kristo.

watoto

" watu wanaoweza kudanganywa kwa urahisi"

Imeandikwa katika sheria

Kwa maneno mengine ni kusema "Nabii aliandika maneno haya katika sheria (Agano la Kale)"

Kwa watu wa lugha nyingine na kwa midomo ya wageni

Vifungu hivi viwili vinamaana moja tu, ili kuweka mkazo.

1 Corinthians 14:22

Sentensi Unganishi

Paulo anatoa maelekezo mahususi kuhusu utaratibu wa kutumia karama katika kanisani.

sio kwa walioamini, bali kwa wasioamini.

Kwa maelezo chanya ni sawa na kusema "kwa waaminio tu"

1 Corinthians 14:24

atashawishiwa na yote asikiayo. Atahukumiwa na yote yasemwayo

Paulo anasema jambo moja mara mbili ili kuweka mkazo. kwa maneno mengine anasema atatambua kuwa anahatia ya dhambi kwa kuwa amesikia mnachosema"

Siri za moyo wake zingefunuliwa

kwa muundo tendaji ni kusema "Mungu angemfunulia siri za moyo wake"

1 Corinthians 14:26

Nini kifuatacho basi,

"kwa sababu kila kitu nilichowaambia ni cha kweli, na hicho ndicho mnapaswa kukifanya"

atafasiri kilichosemwa

katika muundo tendaji ni kusema "tafasirini walichokisema"

kutafasiri...tafasiri

Hii inamaanisha kufafanua kile anachosema mtu kwa lugha isiyofahamika kwa wengine. Anagalia 2:12 kwa maelezo zaidi kuhusu "tafasiri"

1 Corinthians 14:29

manabii wawili au watatu wanene,

inaweza kumaanisha: 1) Manabii wawili au watatu tu wahutubie katika kusanyiko moja au 2)Manabii wawili au watatu tu wapokezane katika kunena kwa wakati mmoja.

kilichosemwa

katika muundo tendaji ni " kile wanachonena"

akifunuliwa jambo

katika muundo tendaji unaweza kusema " Kama Mungu akimpa ufunuo mtu mmoja"

1 Corinthians 14:31

anaweza kutoa unabii mmoja baada ya mwingine

Mtu mmoja tu anaweza kutoa unabii kwa wasaa (watu wawili wasitoe unabii kwa wakati ule ule)

wote waweze kutiwa moyo

kwa muundo tendaji ni kusema "Farijianeni wote kwa pamoja"

Mungu si Mungu wa machafuko,

Mungu huwa haleti machafuko kwa kuwafanya watu wanene(waongee) wote kwa wakati ulele.

1 Corinthians 14:34

wakae kimya

hapa inaweza kumaanisha 1) achani kunena 2) acheni kunena wakati mtu anapotoa unabii au 3) kaeni kimya kabisa wakati wa ibada kanisani

Je neno la Mungu lilitoka kwenu? Je limewafikia ninyi tu?

Paulo anasisitiza kwamba mapenzi ya Mungu kwa Wakristo hakifahamiki kwa waumini wa Korintho peke yake. Kwa maneno mengine ni kusema " Neno la Mungu halikutoka kwenu hapo Korintho; ninyi siyo watu pekee munaofahamu mapenzi ya Mungu.

1 Corinthians 14:37

inampasa ayatambue

Nabii wa kweli au mtu wa kiroho atayakubali maandiko ya Paulo kuwa yanatoka kwa Bwana

mwacheni asitambuliwe

Hapa inaweza kueleza kwa muundo tendaji kuwa "msimtambue mtu huyo"

1 Corinthians 14:39

msimkateze mtu yeyote kunena kwa lugha

Paulo anaweka wazi kuwa kuongea kwa lugha kanisani inawezekana na inakubalika

Lakini mambo yote yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu

Paulo anasisistiza kwamba makusanyiko ya kanisa( waumini) lazima yafanyike katika utaratibu mzuri. kwa maneno mengine " lakini fanyeni mambo yote kwa uzuri na katika utaratibu" au " lakini fanyeni kila kitu kwa utaratibu mzuri, kwa njia inayofaa"

1 Corinthians 15

1 Wakorintho 15 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Ufufuo

Sura hii inajumuisha mafundisho muhimu kuhusu ufufuo wa Yesu. Watu wa Kigiriki hawakuamini kwamba mtu anaweza kuishi baada ya kufa. Paulo anatetea ufufuo wa Yesu. Anafundisha kwa nini ni muhimu kwa waumini wote. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#resurrection and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#believe)

Dhana maalum katika sura hii

Ufufuo

Paulo anaonyesha ufufuo kama ushahidi wa mwisho kwamba Yesu ni Mungu. Kristo ni wa kwanza kati ya wengi ambao Mungu atawafufua. Ufufuo ni muhimu kwa Injili. Mafundisho machache tu ni ya muhimu kama haya.(See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#goodnews and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#raise)

Mifano muhimu za matamshi katika sura hii

Paulo anatumia mifano nyingi za matamshi katika sura hii. Anazitumia kueleza mafundisho magumu ya kitheolojia kwa namna ambayo watu wanaweza kuelewa.

<< | >>

1 Corinthians 15:1

Sentensi Unganishi

Paulo anawakumbusha kuwa ni Injili inayowaokoa na tena anawaeleza Injili ni kitu gani. Kisha anatoa somo fupi la historia kuelezea yatakayotokea hapo baadaye.

Ninawakumbusha

"kuwasaidia ninyi kukumbuka"

kusimama kwayo

Paulo anazungumzia habari ya Wakorintho akiwafananisha na nyumba, na Injili anaifananisha na msingi unaobeba hiyo nyumba

mmeokolewa

Hii inaweza kuelezewa katika muundo tendaji "Mungu atawaokoa"

1 Corinthians 15:3

kwa umuhimu

inaweza kumaanisha 1) muhimu zaidi katika mambo mengi au 2) jambo la kwanza kutokea

kwa ajili ya dhambi zetu

" kulipa kwa ajili ya dhmbi zetu" au " ili Mungu atusamehe dhambi zetu"

kutokana na maandiko

Paulo ana rejea maandiko ya Agano la Kale.

alizikwa

Katika hali tendaji unaweza kusema "Walimzika"

alifufuka

Katika hali tendaji unaweza kusema " Mungu alimfufua" au "alifufuka"

1 Corinthians 15:5

Sentensi unganishi

ukitaka mstari wa (5) uwe sentensi kamili, weka koma kwenye mstari 3 sura ya (15) 15:3, mstari huu wa 5 uweke mbele yake ili kuleta sentensi kamili.

aliwatokea

"alijionyesha mwenyewe kwao"

Mia tano

inamaanisha 500

1 Corinthians 15:8

Mwisho wa yote

"Hatimaye, baada ya kuwa ameonekana kwa wengine"

mtoto aliye zaliwa katika wakati usio sahihi

Paulo anatumia lugha ya nahau na pengine anamaanisha kuwa alimwamini Yesu baadaye sana ukilinganisha na mitume wengine. au anamaanisha kuwa, tofauti na mitume wengine hakushuhudia huduma ya Yesu ya miaka mitatu. kwa maneno mengine "mtu alisiyekuwa na uzoefu walioupata wengine."

1 Corinthians 15:10

kwa neema ya Mungu niko vile nilivyo

neema ya Mungu au wema wa Mungu umemfanya Paulo kuwa kama alivyo.

neema yake kwangu haikuwa bure

Paulo anasisistiza kwa maneno mazuri kwamba Mungu alifanya kazi kupitia kwa Paulo. Kwa maneno mengine ni kwamba " kwa sababu alikuwa mwema kwangu, niliweza kufanya kazi nzuri zaidi"

neema ya Mungu iliyo ndani yangu

Paulo anazungumza juu ya kazi aliyoweza kufanya kwa kuwa Mungu alikuwa mwema kwake, Paulo anasema ilikuwa ni neema iliyokuwa ikifanya kazi ndani yake. Hii inaweza kumaanisha: 1) huu ni ukweli halisi,kuwa Mungu alifanya kazi na kwa wema wake alimtumia Paulo kama chombo au 2) Paulo anatumia sitiari na anasema kuwa Mungu alikuwa mwema kumwezesha Paulo kufanya kazi na kuwezesha kazi za Paulo zifanikiwe vizuri.

1 Corinthians 15:12

iweje baadhi yenu mseme hakuna ufufuo wa wafu?

Paulo anatumia swali hili kuanza mada mpya. Kwa maneno mengine anasema "Hampaswi kuwa mnasema hakuna ufufuo wa wafu"

kama hakuna ufufuo wa wafu, hivyo hata Kristo hajafufuliwa.

Kusema kwamba hakuna ufufuo wa wafu, ni kusema kwamba Kristo hakufufuka kutoka kwa wafu.

1 Corinthians 15:15

Sentensi Unganishi

Paulo anataka kuwathibitishia kuwa Kristo alifufuka kutoka kwa wafu.

Na tumepatikana kuwa mashahidi wa uongo kumuhusu Mungu

Paulo anahoji kwamba kama Kristo hakufufuka kutoka kwa wafu, hivyo wanatoa ushahidi wa uongo kuhusu Kristo kwamba amefufuliwa kutoka kwa wafu.

tumepatikana

"kila mtu anaweza kuona jinsi tulivyo"

imani yenu ni bure na bado mko kwenye dhambi dhambi.

imani yao ni kuwa Kristo alifufuka kutoka kwa wafu, na kama hicho hakikutokea, imani yao haina maana, haiwasaidii chochote.

1 Corinthians 15:18

watu wote

"kila mtu , wote kwa pamoja wanaoamini na wasioamini"

sisi ni wa kuhurumiwa zaidi

"watu lazima watuhurumie zaidi ya ilivyo kwa mwingine yeyote"

1 Corinthians 15:20

sasa Kristo

" hivi ndivyo ilivyo, "Kristo" au " huu ndio ukweli: Kristo"

Kristo amefufuka

katika hali tendaji ni kusema: "Mungu amemfufua Kristo"

1 Corinthians 15:22

Adamu

Adamu alikuwa mtu wa kwanza ambaye aliumbwa na Mungu. Adamu na mke wake Eva waliumbwa katika sura ya Mungu. Mungu alimuumba Adamu kutoka katika mavumbi na kumpulizia pumzi ya uhai.

Kifo, kufa

Maneno haya yametumika kumaanisha kifo cha kimwili na kifo cha kiroho. Kifo cha kimwili inamaanisha mwili wa mtu unapokoma kuwa na uhai. Kifo cha Kiroho, inamaanisha watenda dhambi wanapokuwa wametengwa na Mungu kwa sababu ya dhambi zao.

Kristo

Neno Kristo au Masihi linamaanisha " aliyetiwa mafuta" na neno hili linamhusu Yesu, Mwana wa Mungu.

Hai

Neno hili linamaanisha kuwa na uzima, iliyohai. Wakati mwingine linatumiwa kwa lugha ya picha kuelezea uzima wa kiroho.

matunda ya kwanza

Neno"matunda ya kwanza" linamaana ya sehemu ya mazao,matunda au mboga zilizokuwa za kwanza kuvumwa wakati wa majira ya mavuno. Waisraeli walitoa matunda haya kama sadaka kwa Mungu.

1 Corinthians 15:24

Maelezo ya Jumla

Hapa neno " ata-kapo" ni rejea kwa Kristo.

atakapo komesha utawala wote na mamlaka yote na nguvu

" atawakomesha watu ambao wanatawala, wenye mamlaka, na wenye nguvu ya kufanya yote wanayofanya"

mpaka atakapoweka maadui zake wote chini ya miguu yake

Wafalme walioshinda vita waliweza kuweka miguu yao juu ya shingo za adui zao waliowashinda. Kwa maneno mengine hapa inasema "mpaka Mungu atakapo waharibu kabisa maadui wa Kristo."

Adui wa mwisho kuharibiwa ni kifo

Paulo anaeleza juu ya kifo kana kwamba anaeleza habari za mtu ambaye Mungu atamuua. Kwa maneno mengine ni kusema "Adui wa mwisho ambaye ataharibiwa na Mungu ni kifo chenyewe"

1 Corinthians 15:27

ameweka kila kitu chini ya miguu yake

Wafalme walioshinda vita waliweza kuweka miguu yao juu ya shingo za adui zao waliowashinda. Kwa maneno mengine hapa inasema " Mungu amewaharibu kabisa maadui wote wa Kristo"

vitu vyote vimewekwa chini yake

Maneno haya yakisemwa kwa kauli tendaji ni kwamba " Mungu amavitiisha vitu vyote chini ya Kristo"

mwana mwenyewe atawekwa chini

Maneno haya yakisemwa kwa kauli tendaji ni kwamba " mwana mwenyewe atatiishwa"

mwana mwenyewe

Katika mistari ya awali neno " mwana" linamaanisha " Kristo" : kwa maneno mengine ni kusema " Kristo ambaye ni Mwana wa Mungu"

Mwana...Baba

Hivi ni vyeo muhimu vinavyofafanua uhusiano kati ya Yesu na Mungu.

1 Corinthians 15:29

Au sivyo watafanya nini wale waliobatizwa kwa ajili wafu?

Kwa ufafanuzi Paulo anasema "vinginevyo ingekuwa haina maana kwa Wakristo kubatizwa kwa niaba ya wafu."

kwa nini tena wanabatizwa kwa ajili yao?

Paulo anataka jambo hili lifahamike kwa Wokorintho hata kabla hajalisema kwao ya kwamba " hakuna sababu yoyote kupokea au kubatizwa kwa niaba ya watu walikwisha fariki"

Na kwa nini tuko katika hatari kila saa?

Kwa maneno mengine ni kusema " hatupati faida yoyote kwa kujiweka katika hatari muda wote"

1 Corinthians 15:31

Nakufa kila siku. Hili nalisema kwa kujisifu kwa ajili yenu

" ninajisifu kwa ajili yenu, hivyo kila mmoja anajua kwamba nasema ninaposema ninakufa kila siku"

Ninakufa kila siku.

Paulo anacho maanisha hapa ni (1)kila siku najipambanua kwa kifo cha Kristo kwa kufisha tamaa mbaya ndani yake 2) kila siku aliishi akijua kuwa kuna watu walikuwa wakitafuta kumuua.

Inanifaidia nini..nilipigana na wanyama wakali huko Efeso... hawafufuliwi?

Paulo anataka Wakorintho wafahamu jambo hilo hata bila kuwaambia. kwa maneno mengine anasema " sikupata chochote...kwa kupigana na wanyama huko Efeso... hawafufuliwi"

kama nilipigana na wanyama katika Efeso

Kuna uwezekano maana ni 1) Paulo alikuwa anaongea kwa mfano kuhusu hoja yake na wapagani waliosoma au mafarakano mbalimbali na watu waliotaka kumuua au 2) Anathibitisha kwamba aliwahi kuwekwa kwenye uwanja kupambana dhidi ya wanyama hatari.

Na tule na kunywa, kwa kuwa kesho tunakufa.

Paulo anahitimisha kwamba kama hakuna maisha mengine baada ya kifo, ni bora kwetu kuyafurahia maisha haya kwa kadri tuwezavyo, kwa kuwa kesho maisha yetu yataisha bila matumaini yoyote

1 Corinthians 15:33

Makundi mabaya huharibu tabia njema

Kama ukiishi na watu wabaya, utatenda kama wao. Hapa Paulo ananukuu msemo unaojulikana

Muwe na kiasi

"Mnapaswa kutafakari kwa undani kuhusu hili"

1 Corinthians 15:35

Sentensi unganishi

Paulo anatoa maelezo mahususi juu ya ufufuo wa miili ya waumini utakavyotokea. Anaeleza juu ya miili ya asili na miili ya kiroho kwa kulinganisha Adamu wa kwanza na Aadamu wa mwisho ambaye ni Kristo.

Lakini mtu mwingine atasema, "Jinsi gani wafu wanafufuliwa? Nao watakuja na aina gani ya mwili?"

Hapa inaweza kumaanisha 1)mtu alikuwa akijiho kwa nia njema au) 2) mtu anauliza swali ili kukejeli swala la ufufuo. kwa maneno mengine ni kusema "Baadhi ya watu watasema kwamba hawapati picha jinsi Mungu atakavyo wafufua wafu, na aina gani ya mwili Mungu atawapa katika ufufuo."

mtu mwingine atasema

"mtu atauliza"

Nao watakuja na aina gani ya mwili

hii ni sawa na kuuliza kwamba, je utakuwa mwili halisi au mwili wa kiroho? je mwili huo utakuwa na umbo gani? je mwili huo utatengenezwa kwa vitu gani?

Wewe ni mjinga sana! Kile ulichopanda

Paulo anaonekana kama vile anazungumza na mtu mmoja "Wewe" ni neno kuonyesha umoja.

Wewe ni mjinga

" hujui kabisa kuhusu mambo haya yote"

Kile ulichopanda hakiwezi kuanza kukua isipokuwa kimekufa.

Kama vile mbegu isivyo weza kuota mpaka ifukiwe ardhini. Vile vile mtu lazima afe kwanza kabla ya kufufuliwa na Mungu

1 Corinthians 15:37

kile ulichopanda sio mwili utakaokuwa

Fumbo la mbegu limetumika tena, kumaanisha kwamba mwili wa mkristo uliokufa utafufuliwa na hautaonekana kama ulivyokuwa.

unachopanda

Paulo anaongea na Wakorintho kana kwamba ni mtu mmoja " unachopanda"

Mungu ataipa mwili kama apendavyo

"Mungu ataamua ni mwili wa aina gani"

mwili

Katika mazingira ya wanyama, "mwili" unaweza kutafasiliwa kama "mwili," "ngozi," au "nyama."

1 Corinthians 15:40

miili ya mbinguni

Kunauwezekano maana ni 1) jua, mwezi, nyota, na mianga mingine ionekanayo katika wingu au 2) viumbe vya mbinguni, kama vile malaika na visivyo vya kawaida.

miili ya duniani

Hii ina rejea kwa wanadamu.

utukufu wa miili ya mbinguni ni wa aina moja na na utukufu wa ulimwenguni ni mwingine.

"utukufu uliopo katika miili ya mbinguni ni tofauti na utukufu uliopo katika miili ya asili ya wanadamu "

utukufu

Hapa "utukufu" unafananishwa na mfano wa mwangaza wa vitu vya angani katika jicho la mwanadamu.

1 Corinthians 15:42

Kinacho pandwa..., na kinacho ota...

Mwandishi anafananisha watu wanaozika maiti kwenye kaburi na watu wanaopanda mbengu itakayo zaa matunda. kwa kitenzi tendaji ni sawa na kusema " Ni kipi kinazikwa kaburini... nikipi kinachotoka kaburini " au watu huzika kitu gani...na Mungu hufufua kitu gani"

kinaharibika... hakiharibiki.

Kina oza... kisichoweza kuoza

1 Corinthians 15:45

Lakini wa kiroho hakuja kwanza bali wa asili, na kisha wa kiroho.

" mtu wa asili alikuja kwanza. mtu wa kiroho alikuja baadaye na anatoka kwa Mungu"

asili

aliumbwa kwa namna ya kidunia, na bado hajawa katika mahusiano na Mungu.

1 Corinthians 15:47

Mwanadamu wa kwanza ni wa dunia, alitengenezwa kwa mavumbi

hapa inaelezea kuwa Mungu alimuumba mtu wa kwanza (Adamu) kutoka katika mavumbi ya ardhi

vumbi

" uchafu"

mtu wa mbinguni

Yesu Kristo

wale ambao ni wa mbinguni

"wale wanaomwamini Kristo"

tumebeba

"kubali kuchukua na kuakisi"

1 Corinthians 15:50

Sentensi unganishi

Paulo anataka wajue kuwa baadhi ya waumini hawatakufa kimwili bali watapata mwili wa ufufuo kupitia ushindi wa Kristo

kwamba mwili na damu haviwezi kuurithi ufalme wa Mungu

maana zinazokubalika ni: 1) sentensi zote mbili zinamaanisha jambo moja. " Mwanadamu ambao watakufa kabisa hawawezi kuurithi ufalme wa Mungu unaodumu daima" au 2) sentensi ya pili inakamilisha lile wazo linalotangulia hapo mwanzo, kuwa " wanadamu waliodhaifu hawawezi kuurithi ufalme wa Mungu. Wala ambao watakufa hawataweza kuurithi ufalme wa Mungu ambao utadumu milele"

mwili na damu

Ni wale wanafuata tabia za mwili uliohukumiwa kufa.

kurithi tutabadilishwa wote

Ni hali ya kupokea mambo ambayo Mungu ameahidi kwa waumini na Paulo anazungumzia jambo hili kama vile mtu anavyopata urithi wa mali na utajiri kutoka kwa mwanafamilia : "Mungu atatubasilisha sisi sote"

wakuharibika...wakutoharibika

"unaoweza kuoza....usioweza kuoza wala kuharibika"

wote tutabadilishwa

Hii inaonyesha hali tendaji kuwa " Mungu atatubadilisha sisi sote"

1 Corinthians 15:52

Tutabadilishwa

"Mungu atatubadilisha"

katika kufumba na kufumbua kwa jicho

Itatokea kwa haraka kama vile mtu anavyo kufunga na kufungua jicho lake.

katika tarumbeta ya mwisho

"tarumbeta ya mwisho itakapolia"

hali ya kutoharibika

"umbo ambalo halitaharibika ... mwili huu unaweza kuharibika(kuoza).Kupingwa kwa mbiu kunatanguliza matukio makubwa. Katika swala hili, Paulo ana rejea kwenye tukio kubwa la mwisho katika historia ya dunia hii.

huyu binadamu lazima awekwe kwenye milele

Paulo anazungumzia juu ya Mungu kuibadilisha miili yetu ili isife tena ni kana kwamba Mungu anaweka mavazi mapya kwetu.

1 Corinthians 15:54

huu mwili wa kuhalibika...na usioharibika

"mwili huu unaweza kuoza... usioweza kuoza" angalia tafasiri inayofanana na hii katika 15:42

Kifo, ushindi wako uko wapi? Kifo, uko wapi uchungu wako?"

Paulo anasema haya kufanya dhihaka dhidi ya nguvu ya kifo ambayo tayari Kristo amekwisha kuishinda. kwa maneno mengine ni kwamba: " Kifo hakina ushindi. Kifo hakina makali."

1 Corinthians 15:56

Uchungu wa kifo ni dhambi

Ni kwasababu ya dhambi tutakabiliwa na kifo, hivyo tunakufa.

nguvu ya dhambi ni sheria

Sheria ya Mungu iliyopitishwa na Musa inafafanua juu ya dhambi na inatuonyesha jinsi tunavyotenda dhambi dhidi ya Mungu.

atupaye sisi ushindi

" amekwisha kushinda kifo kwa niaba yetu"

1 Corinthians 15:58

Sentensi unganishi

Paulo anataka waumini wakati wanamtumikia Bwana wakumbuke juu ya kugeuzwa na kupata miili ya ufufuo ambayo Mungu atawapatia.

iweni imara na msitikisike.

Paulo anaelezea juu mtu mwenye nguvu za kimwili asiyekubali kushindwa katika kutimiza uamuzi wake. kwa maneno mengine inamaanisha " kufanya uamuzi thabiti"

Daima itendeni kazi ya Bwana

Paulo anaongelea jitihada alizifanya katika kumtumikia Bwana kama vile vitu vya thamani ambavyo kila mtu anapaswa kuvipata. kwa maneno mengine anasema " siku zote mtumikieni Bwana kwa uaminifu"

1 Corinthians 16

1 Wakorintho 16 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Paulo anaeleza kwa kifupi mada nyingi katika sura hii. Ilikuwa ni kawaida katika inchi za kale za Mashariki ya Karibu kwa sehemu ya mwisho ya barua kuwa na salamu za kibinafsi.

Dhana maalum katika sura hii

Maandalizi ya kuja kwake

Paulo alitoa maelekezo ili kusaidia kanisa la Korintho kujitayarisha kwa Paulo kuwatembelea. Aliwaambia waanze kukusanya fedha kila Jumapili kwa ajili ya waumini huko Yerusalemu. Alikuwa na matumaini ya kuja na kukaa pamoja nao wakati wa msimu wa baridi. Aliwaambia wamsaidie Timotheo atakapofika. Alikuwa na matumaini kuwa Apollo angewatembelea, lakini Apolo hadhani kwamba ilikuwa wakati mzuri. Paulo pia aliwaambia wamtii Stephanus. Kwa mwisho, alituma salamu kwa kila mtu.

__<< | __

1 Corinthians 16:1

Sentensi unganishi

Paulo anawakumbusha waumini wa Korintho kukusanya pesa kwa ajili ya waumini wenye mahitaji walioko Yerusalemu. Pia anawajulisha kuwa Timotheo atapitia kwao kabla ya kwenda kwa Paulo.

ya waumini

Paulo alikuwa anakusanya pesa kutoka kwenye makanisa yake kwa ajili ya wakristo masikini wa kiyahudi huko Yerusalemu na Yuda.

kama nilivyo elekeza

"kama nilivyowapa maelekezo mahususi"

aweke kitu fulani kando na kukihifadhi,

Maana zinazowezekana ni: 1) " kitu hicho tunza nyumbani" au 2) "kilete kitunzwe kanisa"

ili kwamba kusiwe na makusanyo wakati nitakapokuja

" kwa hiyo nitakapokuja hakutakuwa na haja ya kukusanya pesa zingine zaidi"

1 Corinthians 16:3

yeyote mtakayemchagua

Paulo anawajulisha kanisa kwamba wanaweza kuteua baadhi ya watu miongoni mwao ili kupeleka sadaka zao Yerusalemu. "yeyote mtakaye mchagua" au " watu mtakaowateua"

nitamtuma pamoja na barua

Maana inayowezekana ni: 1) "Nitatuma na barua ambayo nitaiandika" au 2) "Nitatuma na barua ambayo mtaiandika."

1 Corinthians 16:5

mnaweza kunisaidia katika safari yangu

Hii inamaanisha kwamba wangeweza kutoa fedha au vitu mbalimbali anavyohitaji alivyohitaji Paulo na watumishi wenzake ili waweze kuendelea na safari yao.

1 Corinthians 16:7

kuwa sitarajii kuwaona sasa

Paulo anaeleza kwamba hataki kuwa na ziara ya ya muda mfupi, lakini anapenda kufanya ziara yamuda mrefu hapo baadaye.

Pentekoste

Paulo alitarajia kubakia Efeso hadi sikukuu, iliyoanza mwezi Mei au Juni, siku hamsini baada ya pasaka. Baada ya hapo angesafiri kupitia Makedonia, na kufika Korintho kabla ya majira ya baridi yalioanza mwezi wa Novemba

mlango mpana umefunguliwa

Hii inamaanisha kwamba Mungu amempa nafasi nzuri ya kuwafikia watu kwa injli.

1 Corinthians 16:10

muoneni kwamba yuko na ninyi pasipo kuogopa

" kusiwe na sababu ya kumfanya aogope anapokuwa miongoni mwenu"

Mtu yeyote asimdharau

Timotheo alikuwa kijana sana kuliko Paulo hivyo wakati mwingine hakupewa heshima aliyostahili kama mtumishi wa Injili

ndugu yetu Apolo

Neno "yetu" nilinamhusu Paulo na watu aliowaandikia

1 Corinthians 16:13

Muwe macho, simameni imara, mtende kama wanaume, muwe na nguvu

Paulo anawasisitiza Wakorintho kwa kuwapa maelekezo kana kwamba anatoa amri nne kwa askari wa vita. Hizi amri nne zinamaanisha jambo lilelile.

Muwe macho

Paulo anawaambia watu watambue mambo yanayotokea kama vile walinzi wavyokaa macho wanapolinda mji au Shamba. kwa maneno mengine anasema "muwe makini sana kuhusu kwa yeyote mnayemwamini" au " jilindeni na hatari yoyote"

simameni imara

Paulo anawahimiza waendelee kuamini katika Kristo kulingana na mafundisho yake, wawe kama askari wasiokubali kurudi nyuma wanaposhambuliwa na adui. hii inamaana: 1) " endeleeni kuamini kile tulichowafundisha" au 2) " endeleeni kumwamini Kristo kwa udhabiti wote"

mtende kama wanaume

katika nyakati alizoishi Paulo na watu aliowaandikia barua yake, ilikuwa kawaida kwa wanaume kufanya kazi ngumu kwa ajili ya mahitaji ya familia na kupigana dhidi ya maadui. kwa uwazi zaidi inamaanisha " timizeni wajibu wenu"

yote myafanyayo yafanyike katika upendo

"lazima kila jambo mnalolifanya lioneshe kuwa mnaupendo kwa watu"

1 Corinthians 16:15

Sentensi unganishi

Paulo anaanza kutuma salamu zake anapoelekea kuhitimisha barua yake, anatoa salamu za makanisa mengine, Prisca, Akila na yeye mwenyewe.

kaya ya Sefana

Stefana alikuwa muumini wa kwanza katika kanisa la Koritho.

Akaya

Akaya ni jina la jimbo la Ugiriki

1 Corinthians 16:17

Stefana, Fotunato, na Akiko

Hawa watu pengine walikuwa baadhi ya waumini wa kwanza wa Korintho au wazee wa kanisa ambao waliokuwa watendakazi pamoja na Paulo.

Stefana, Fotunato, na Akiko

Haya ni majina ya watu

Wamesimama mahali ambapo ninyi mgepaswa kuwa

" walisababisha mafanikio yawepo japo ninyi hamkuwepo"Paulo alitiwa moyo kwa ujio wao.

Kwa kuwa wameifurahisha roho yangu

"Paulo alitiwa moyo walipokuja kumtembelea"

1 Corinthians 16:19

Kanisa

katika agano jipya neno " kanisa" lina maana ya kundi la watu wanaomwamini Yesu ambao walikutana pamoja kuomba na kusikia mahubiri ya neno la Mungu. Mara nyingi Neno "kanisa" linamaanisha wakristo wote.

Asia

Nyakati za Biblia, "Asia" ilikuwa ni jina mkoa au jimbo katika dola la Warumi. Hii sehemu ilikuwa upande wa magharibi na kwa sasa inajulikana kama nchi ya Utiruki. Miji kama Efeso, na Kolose ilikuwa katika eneo hili la Asia ambapo Paulo alisafiri na kuhubiri injili.

Akila

Akila alikuwa mkristo wa Kiyahudi kutoka katika jimbo la Ponto, mkoa wa kusini mwa pwani ya bahari nyeusi().

Priska

Priska alikuwa mke wa Akila yeye na mume wake walikuwa wakristo waliofanya kazi ya umisheni pamoja na mtume Paulo.

Bwana

Neno" Bwana" linamaana y mtu mwenye kumikili au mamlaka juu ya watu. Neno hili linapoandikwa kwa herufi kubwa humaanisha Mungu.

takatifu

Neno "takatifu" huzungumzia tabia ya Mungu ambayo ni kamilifu na imejitenga mbali na dhambi. ni Mungu pekee ambaye ni mtakatifu, huwa anawafanya watu na vitu kuwa watakatifu

busu

Busu ni tendo la mtu kuweka mdomo wake kwenye mdomo wa mtu mwingine. Katika Biblia neno hili busu wakati mwingine limetumika kumaanisha kuagana au kuwambia mtu kwahari.

1 Corinthians 16:21

Mimi, Paulo, naandika hivi kwa mkono wangu

Paulo alikuwa anaweka wazi kuwa maelekezo katika ile ya barua alitoka kwake, ingawa Paulo alikuwa akisema na matendakazi mwenza aliandika yale maneno yake. Sehemu ya mwisho wa barua Paulo akaiandika kwa mko wake mwenyewe.

laana iwe juu yake.

"Mungu anaweza kumlaani" angalia tafasiri ya neno laana katika 12:1

Utangulizi wa 2 Wakorintho

Sehemu ya 1: Utangulizi wa Ujumla

Maelezo ya Kitabu cha 2 Wakorintho

  1. Paulo anashukuru Mungu kwa Wakristo wa Korintho (1:1-11)
  2. Paulo anaelezea mwenendo wake na huduma yake (1:12-7:16)
  3. Paulo anaongea kuhusu kuchangia fedha kwa kanisa la Yerusalemu (8:1-9:15)
  4. Paulo anatetea mamlaka yake kama mtume (10:1-13:10)
  5. Paulo anatoa salamu za mwisho na himizo (13:11-14)

Nani aliandika Kitabu cha 2 Wakorintho?

Paulo aliandika 1 Wakorintho. Paulo alitoka mji wa Tarso. Alikuwa anajulikana kama Sauli katika maisha yake ya awali. Kabla ya kuwa Mkristo, Paulo alikuwa Mfarisayo. Aliwatesa Wakristo. Baada ya kuwa Mkristo, alisafiri mara kadhaa katika Ufalme wa Roma akiwaambia watu kuhusu Yesu.

Paulo alianzisha kanisa lililokutana huko Korintho. Alikuwa akiishi katika mji wa Efeso wakati aliandika barua hii.

Je, kitabu cha 2 Wakorintho kinahusu nini?

Katika 2 Wakorintho, Paulo aliendelea kuandika juu ya migogoro kati ya Wakristo katika jiji la Korintho. Ni wazi katika barua hii kwamba Wakorintho walikuwa wametii maelekezo yake ya awali kwao. Katika 2 Wakorintho, Paulo aliwahimiza kuishi kwa njia ambayo ingeweza kumpendeza Mungu.

Paulo pia aliwaandikia kuwahakikishia kwamba Yesu Kristo alimtuma awe mtume kuhubiri Injili. Paulo alitaka waelewe jambo hilo, kwa sababu kundi la Wakristo wa Kiyahudi walipinga kile alichokifanya. Walisema Paulo hakutumwa na Mungu na alikuwa akifundisha ujumbe wa uwongo. Kundi hili la Wakristo Wayahudi walitaka Wakristo wasio Wayahudi kutii sheria ya Musa.

Je, kichwa cha kitabu hiki kinapaswa kutafsiriwaje?

Watafsiri wanaweza kuchagua kuita kitabu hiki kwa kichwa chake cha jadi, "Wakorintho wa Pili." Au wanaweza kuchagua kichwa wazi, kama "Barua ya pili ya Paulo kwa Kanisa la Korintho." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-names)

Sehemu ya 2: Dhana muhimu za Kidini na za Kitamaduni

Mji wa Korintho ulikuwaje?

Korintho ilikuwa mji mkuu katika Ugiriki wa kale. Kwa sababu ulikuwa karibu na Bahari ya Mediterane, wasafiri wengi na wafanyabiashara walikuja kununua na kuuza bidhaa huko. Hii ilisababisha mji kuwa na watu kutoka tamaduni nyingi tofauti. Mji huo ulijulikana kwa kuwa na watu waliokuwa wameishi katika njia za uasherati. Watu waliabudu Afrodito, mungu wa kike wa upendo wa Kigirik. Kama sehemu ya sherehe za kuheshimu Afrodito, waabudu wake walifanya ngono na makahaba wa hekalu.

Paulo alimaanisha nini kwa "mitume wa uongo" (11:13)?

Hawa walikuwa Wakristo wa Wayahudi. Walifundisha kwamba Wakristo wa Mataifa walipaswa kutii sheria ya Musa ili kufuata Kristo. Waongozi wa Kikristo walikutana huko Yerusalemu na kuamua juu ya jambo hilo (Angalia: Matendo 15). Lakini, ni wazi kwamba kulikuwa tena makundi kadhaa ambayo walikataa kile kilichoamuriwa na waongozi wa Yerusalemu.

Sehemu ya 3: Masuala muhimu ya Tafsiri

"Umoja na wingi wa neno "you"

Katika kitabu hiki, neno "mimi" linamaanisha Paulo. Pia, neno "nyinyi" ni karibu kila mara kwa wingi na linamaanisha waumini huko Korintho. Lakini, kuna tofauti mbili kati ya misitari ya 6:2 na 12:9. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-exclusive and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-you)

Je, mawazo ya "takatifu" na "kutakasa" yanawakilishwaje katika 2 Wakorintho kwenye ULB?

Maandiko hutumia maneno kama hayo ili kuonyesha moja ya mawazo mbalimbali. Kwa sababu hii, mara nyingi ni vigumu kwa watafsiri kuyawakilisha vizuri katika tafsiri zao. Katika kutafsiri kwa Kiingereza, ULB inatumia kanuni zifuatazo:

Mara nyingi UDB husaidia watafsiri kufikiri juu ya jinsi ya kuwakilisha mawazo haya katika tafsiri zao wenyewe.

Paulo alimaanisha nini kwa maneno "katika Kristo" na "katika Bwana"?

Maneno haya hutokea katika 1:19, 20; 2:12, 17; 3:14; 5:17, 19, 21; 10:17; 12:2, 19; na 13:4. Paulo alijaribu kueleza wazo la muungano wa karibu kati ya Kristo na waumini. Lakini, mara nyingi alitaka kuelezea maan nyingine pia kwa wakati huo huo. Kwa mfano, angalia, "Mlango ulifunguliwa kwangu katika Bwana," (2:12) ambako Paulo alinamaanisha kuwa mlango ulifunguliwa kwa Paulo naye Bwana.

Tafadhali angalia utangulizi wa Kitabu cha Warumi kwa maelezo zaidi juu ya aina hii ya kujieleza.

"Kuwa kiumbe kipya" katika Kristo" kuna maana gani (5:17)

Ujumbe wa Paulo ni kwamba Mungu hufanya Wakristo kuwa sehemu ya "ulimwengu mpya" wakati mtu anaamini Kristo. Mungu anatoa ulimwengu mpya wa utakatifu, amani, na furaha. Katika ulimwengu huu mpya, waumini wana asili mpya ambayo wamepewa na Roho Mtakatifu. Watafsiri wangejaribu kuelezea wazo hili.

Je, kuna masuala gani muhimu katika Kitabu cha 2 Wakorintho?

(See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/jit.html#translate-textvariants)

2 Corinthians 1

2 Wakorintho 01 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Kifungu cha kwanza kinaonyesha njia ya kawaida ya kuanzisha barua katika inchi ya kale ya Mashariki ya Karibu.

Dhana maalum

Uadilifu wa Paulo

Watu walikuwa wanamkosoa Paulo na kusema kuwa yeye hakuwa wa dhati. Anawakemea kwa kuelezea nia zake kwa kile alichokifanya.

Faraja

Faraja ni neno kuu ya sura hii. Roho Mtakatifu huwafariji Wakristo. Pengine Wakorintho walikuwa wanasumbuliwa na walihitaji kufarijiwa.

Mifano muhimu za matamshi katika sura hii

Swali la uhuishaji

Paulo anatumia maswali mawili ya uhuishaji ili kujitetea dhidi ya madai yasiyokuwa ya kweli. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-rquestion)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Sisi

Paulo anatumia neno "sisi". Hii inawezekana kuwakilisha Timotheo na yeye mwenyewe. Inaweza pia kuwajumuisha watu wengine.

Dhamana

Paulo anasema kuwa Roho Mtakatifu ni dhamana, ambayo ina maana ya ahadi au malipo ya kwanza, ya maisha ya Milele ya Mkristo. Wakristo wanaokolewa salama. Lakini hawatapata ahadi zote za Mungu mpaka baada ya kufa. Roho Mtakatifu ni dhamana ya kibinafsi kwamba haya yatafanyika. Wazo hili linatoka kwa tamko la biashara. Mtu hutoa kitu cha bei kubwa kwa mtu mwingine kama "dhamana" kwamba watalipa pesa zote baadaye. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#eternity and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#save)

| >>

2 Corinthians 1:1

Sentensi unganishi

Baada ya salamu za Paulo kwa Kanisa la Korintho, anaandika kuhusu mateso yake na faraja yake kupitia Yesu Kristo. Timotheo yuko pamoja naye pia.

Maelezo ya jumla

Neno "ninyi" katika barua hii ina maanisha watu wa kanisa la Korintho na kwa wakristo wengine katika eneo hilo. Inawezekana Timotheo anaandika kwenye karatasi iliyotengenezwa kwa ngozi mameno anayoyasema Paulo.

Huyu Paulo

Lugha yako inaweza kuwa hasa njia ya kumtambulisha mwandishi wa barua. AT: "Mimi, Paulo, niliandika barua hii."

kaka

Katika Agano Jipya, mtume Paulo mara nyingi alitumia neno "kaka" kumaanisha kwa wakristo wenzangu, kwa kuwa waumini wote katika Kristo ni watu wa familia moja ya kiroho, na Mungu kama Baba yao wa mbinguni.

Akaya

Hili ni jina la jimbo la Kirumi kusini mwa sehemu iitwayo Ugiriki kwa sasa.

Neema iwe kwenu na amani

Neno "kwenu" ina maanisha watu wa kanisa la Koritho na kwa wakristo wengine katika eneo hilo. Hii nisalamu ya kawaida ya Paulo katika barua hizi.

2 Corinthians 1:3

Mungu na baba wa Bwana wetu Yesu Kristo atukuzwe

Hii inaweza kusemwa katika hali tendaji. Tumtukuze Mungu na baba wa Bwana wetu Yesu Kristo daima"

Mungu na Baba

"Mungu, ambaye ni Baba"

Baba wa rehema na Mungu wa faraja yote

Tungo hizi mbili zinaelezea wazo linalofanana katika njia mbili tofauti. Kwa pamoja tungo zinamwelezea Mungu.

Baba wa rehema na Mungu wa rehema na Mungu wa faraja yote

Maana zake zaweza kuwa 1) maneno "rehema" "faraja yote" yanaelezea tabia ya "Baba" na "Mungu" au 2) kwamba maneno "Baba" na "Mungu" yanamwelezea mmoja aliye asili ya "rehema" na "faraja yote."

hutufariji katika mateso yote

Hapa "sisi" na "yetu" hujumlisha Wakorintho.

2 Corinthians 1:5

Kama vile mateso ya Kristo yalivyoongezeka kwa faida yetu

Paulo anazungumzia mateso ya Kristo kama vile yalivyokuwa kielelezo ambacho kingeongezeka katika idadi "Kama vile Kristo alivyoteswa sana kwa faida yetu"

Mateso ya Kristo

Maana zake zaweza kuwa 1) kwamba hii ina maanisha mateso ya Paulo na Timotheo waliyoyapitia kwa sababu wanahubiri ujumbe unaomhusu Kristo au 2) inamaanisha mateso ya Kristo aliyoyapitia kwa niaba yao.

Faraja yetu inadumu

Paulo anazungumza kuhusu faraja kwa vile kama mfano ambao ungeweza kuongezeka ukubwa wake.

lakini kama tukiteswa

hapa neno "sisi" lina maanisha Paulo na Timotheo, lakini siyo Wakorintho. Hii inaweza kuelezwa katika kauli tendaji "Lakini hata kama watu wakitutesa"

Kama tukitiwa faraja

Hii inaweza kuelezwa katika kauli tendaji badala yake " Kama Mungu akitufariji"

Faraja yenu inafanya kazi vizuri

"Mnapitia faraja timilifu"

2 Corinthians 1:8

hatutaki mwe wajinga

Hii inaweza kuelezwa kwa msamiati chanya "tunataka mfahamu"

Tuliteswa sana zaidi ya vile ambavyo tungeweza kuvumilia

Paulo na Timotheo wanaelezea hisia zao za kukata tamaa kama mzigo mzito waliopaswa kuubeba.

Tulikuwa tumekatishwa tamaa kabisa

neno "katishwa tamaa" linaeleza hisia za kuvujwa moyo. Hii inaweza kuelezwa katika muundo wa utendaji. " taabu tulizozipitia zimetukatisha tamaa kabisa" au "Tulikuwa katika kukatishwa tamaa kabisa"

Tulikuwa na hukumu ya kifo juu yetu

Paulo na Timotheo wanalinganisha hisia zao za kuvujwa moyo kama mtu ambaye ametiwa hatiani kufa." " Tulikuwa katika kukata tamaa kama mtu aliyehukumiwa kufa"

lakini badala yake katika Mungu

Maneno "weka tumaini letu" yameachwa katika sentensi hii. "lakini badala yake, weka tumaini letu katika Mungu"

anaye wafufua wafu

"anaye waleta wafu kurudi katika uhai tena"

maafa ya mauti

Paulo na Timotheo wanafananisha hisia yao ya kukata tamaa na maafa ya mauti au hatari ya kutisha. (UDB) AT: "kukata tamaa."

2 Corinthians 1:11

Atafanya hivi kama ninyi pia mlivyotusaidia

"Mungu atatuokoa kutoka hatarini kama ninyi, watu wa kanisa la Korintho, mtusaidia na sisi pia"

Upendeleo wa utukufu umetolewa kweyu

Hii inaweza kuelezwa katika kauli tendaji. "Upendeleo wa utukufu ambao uliotolewa kwetu"

2 Corinthians 1:12

Tunaona fahari juu ya hili..sababu yenu ya kujisifu

"Maneno "kujisifu" na kuona fahari " yametumika hapa katika mtazamo chanya wa utoshelevu wa hisia kubwa na furaha katka kitu fulani.

ushuhuda wa dhamiri zetu

Fikra za Paulo na Timotheo kuhusu matendo yao yashuhudia kwamba wameishi katika njia impendezayo Mungu.

siyo katika hekima ya kidunia

Neno "ya kidunia" linaeleza kile kinachotambulisha jamii ya wanadamu ambayo haimchi Mungu. "siyo kwa kufuata hekima ya kibinadamu"

hatuwaandikii chochote msichoweza kukisoma au kukielewa

Hii inaweza kuelezwa kuwa "Mnaweza kukisoma na kukielewa kila kitu tunachowaandikieni"

kama vile mtakavyokuwa wetu

"Unaweza kuyagawa maneno "Sababu yetu kuona fahari" kujaza duaradufu. "kama mtakavyokuwa sababu yetu ya kuona fahari"

2 Corinthians 1:15

Sentensi unganishi

Paulo anaeleza matumaini yake ya hakika kwa hamasa safi kuja kuwaona waumini katika Korintho baada ya barua yake ya kwanza.

Maelezo ya jumla

Paulo aliandika takribani barua 3 kwa Wakorintho.barua 2 tu kwa Korintho zimeandikwa katika Biblia.

Kwa sababu nilikuwa mwenye ujasiri kuhusu hili

Neno "hili" linaelezea maneno ya mwanzo ya Paulo kuhusu Wakorintho.

mtaweza kupokea faida ya ziara zangu mbili

mtaweza kunufaika kutoka kwangu nitakapowatembelea mara ya pili.

mnitume kwa safari yangu ya Uyahudi

Mniwezeshe kwa safari yangu ya Uyahudi

2 Corinthians 1:17

nilikuwa mashaka?

Paulo anatumia swali hili kusisitiza alikuwa na uhakika uamuzi wake kuwatembelea Wakorintho. Jibu lililotarajiwa kwa swali hili lilikuwa "Nilikuwa sina mashaka" au " Nilikuwa na ujasiri katika uamuzi wangu"

Je, ninapanga vitu kwa mujibu wa vigezo vya kibinadamu kwa wakati mmoja?

Hii ina maanisha kuwa Paulo hakusema kwa pamoja kwamba angetembelea na kwamba asingetembelea. Maneno "ndiyo" na " hapana" yamerudiwa kwa msisitizo. "Kwa hiyo nitasema "Ndiyo" wakati nitakapojuwa kwa hakika kuwa nitatembelea na "Hapana" pale tu ninapojua kuwa sina uhakika wa kutembelea kwa wakati mmoja"

2 Corinthians 1:19

Kwa maana Mwana wa Mungu... siyo "Ndiyo" na "Hapana." Badala yake yeye ni "Ndiyo" daima."

Yesu husema "Ndiyo" daima kuhusiana na ahadi za Mungu, ambazo zinamaanisha kwamba anathibitisha kwamba wako sahihi . Kwa kuwa Mwana wa Mungu ...hasemi " Ndiyo" na " Hapana "kuhusina na ahadi za Mungu. Badala yake husema "Ndiyo" daima

Mwana wa Mungu

Hiki ni cheo muhimu cha Yesu ambacho kinaelezea uhusano kwa Mungu

ahadi zote za Mungu ni "ndiyo" katika yeye

Hii ni kumaanisha kwamba Yesu anahakikisha anatimiza yote yale ambayo Mungu ameahidi katika Kristo Yesu. "Ahadi zote za Mungu zinathibitishwa katika Yesu Kristo"

"Ndiyo" katika yeye...kupitia yeye

Neno "yeye" linarejea kwa Yesu Kristo.

2 Corinthians 1:21

Mungu hututhibitisha sisi na ninyi

Maana zake zaweza kuwa 1)" Mungu ambaye huthibitisha uhusiano wetu na kila mmoja wetu kwa sababu tiko ndani ya Kristo" au 2)"Mungjambaye huthibitisha pamoja uhusiano wetu na wenu pamoja na Kristo."

Ameweka muhuri wake juu yetu

Hii Ina maanisha kwamba Mungu ametutia amewawekea alama wakristo kama miliki yake ."Ametuwekea alama kuwa mali yake"

Ametupa Roho ndani ya mioyo yetu

Hapa neno "Roho" linaeleza utu wa ndani wa mwanadamu. " Ametupa :Roho" kuishi ndani mwa kila mmoja wetu"

Roho ...kama uthibitisho

Roho amezungumzwa kama malipo kuelekea uzima wa milele.

2 Corinthians 1:23

Ninamwita Mungu kubeba ushahidi kwa ajili yangu

Maneno haya "kubeba ushahidi" yana rejea kwa mtu anayesema ambacho wameona au kusikia ili kwamba kutuliza hoja. "Namuuliza Mungu kuonyesha kile ninachosema ni kweli"

Ili kwamba niwahifadhi ninyi

"Ili kwamba nisije kuwafanya kuteseka zaidi"

Tunatenda kazi paoja nanyi kwa ajili ya furaha yenu"

"Tunatenda kazi paoja nanyi ilikwamba muwe na furaha"

Simameni katika imani

Neno "Simameni" linaweza kumaanisha kitu ambacho hakiwei kubadilika. "iweni thabiti katika imani yenu"

2 Corinthians 2

2 Wakorintho 02 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum

Uandishi wa hasira

Katika sura hii, Paulo anaelezea barua aliyowaandikia Wakorintho hapo awali. Barua hiyo ilikuwa na sauti kali na ya kurekebisha. Paulo labda aliandika barua hiyo baada ya barua inayojulikana kama Wakorintho wa Kwanza na kabla ya barua hii. Anasema kuwa kanisa lilipaswa kumkemea mwanachama mkosaji. Paulo sasa anawahimiza kuwa na neema kwa mtu huyo. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#grace and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Harufu

Harufu nzuri inapendeza. Maandiko mara nyingi hueleza mambo ambayo yanampendeza Mungu kama kuwa na harufu nzuri.

<< | >>

2 Corinthians 2:1

Sentensi unganishi

Kwa sababu ya pendo kuu kwa ajili yao, Paulo anaweka wazi kwamba hilo onyo lake katika barua yake ya kwanza kwao(onyo la kukiri dhambi ya uzinzi) ilimsababishia yeye maumivu kama yalivyo maumivu kwa watu wa kanisa katika Korintho na watu wasio na maadili.

Niliamua kwa upande wangu

"Nilifanya uamuzi"

kama niliwasababisha maumivu, ni nani atakayenifurahisha isipokuwa yule niliye muumiza?

Paulo anatumia swali hili la kujihoji kusisitiza kuwa siyo yeye au wao wangenufaika kama kuja kwake kwao kungewasababishia maumivu. " Kama niliwasababishia maumivu , mmoja pekee ambaye angenifurahisha angekuwa ni yule ambaye ambaye aliumizwa nami"

Mmoja pekee aliyeumizwa nami

Hii inaweza kufafanuliwa katika kauli tendaji "yule ambaye aliumizwa nami"

2 Corinthians 2:3

Niliandika kama nilivyofanya

Hiki kinarejea barua nyingine ya Paulo aliyokuwa ameiandika kwa wakristo wa Korintho ambaye haipo." Niliandika kama nilivyofanya katika barua zangu za awali"

Nisingeumizwa na wale waliopaswa kunifanya mimi nifurahi

Paulo anazungumzia kuhusu mwenendo wa baaadhi ya wakristo wa Korintho waliomsababishia yeye maumivu ya kisaikolojia .Hiki kinaweza kuelezwa kwajinsi ya kauli tendaji " wale wliopaswa kunifanya mimi nifurahi wasingeniumiza"

fuaha yangu ni ni furaha ile ile mliyo nayo nyote

"Kile kinachonipa mimi kufurahi ni kile kile kinachowapa ninyi furaha pia"

kutoka katika "mateso" makubwa

Hapa neno "mateso" linaelezea maumivu ya hisia

kwa dhiki ya moyo

Sehemu hii neno "moyo" linamaanisha mahali pa hisia." na huzuni kubwa"

na kwa machozi mengi

"na kwa kulia kwingi"

2 Corinthians 2:5

katika vipimo vingine

"katika baadhi ya sehemu"

bila kuweka uchungu zaidi

" maana zinazopendekezwa ni 1) "Sipendi niseme kwa ukali sana" au 2) Sipendi kulikuza."

Kuhukumiwa kawa mtu yule na watu wengi inatosha

Hii inawea kuelezwa kwa kwa kauli tendaji. Neno " hukumu" linaweza kutafsiriwa kutumia kitenzi. " Kwa jinsi watu wengi walivyomwadhibu mtu huyu inatosha"

inatosha

ni ya kuridhisha

hajatetereshwa na wingi wa huzuni

Ina maanisha kuwa na mwitikio dhabiti wa hisia kwa huzuni nyingi. "huzuni nyingi haziwezi kumwogopesha"

2 Corinthians 2:8

Sentensi Unganishi

Paulo analitia moyo kanisa katika Korintho kuonyesha pendo na kuwasamehe watu wale ambao wamewahukumu. Anaandika kwamba, yeye pia amemsamehe yeye.

thibitisheni pendo lenu hadharani kwa kwa ajili yake

Ina maanisha kwamba wanapaswa kuthibitisha pendo lao kwa ajili ya mtu huyu mbele ya wakristo wote.

ninyi ni watii katika kila jambo

maana pendekezwa ni hizi 1)" ninyi ni watii kwa Mungu katika kila kila kitu" au 2) "ninyi mna utii katika kila jambo nililo wafundisha"

2 Corinthians 2:10

mmesamehewa kwa ajili yenu

"nisamehewa kwa faida yenu." au "mmesamehewa kwa faida yenu"

mmesamehewa kwa faida yenu

"nimesamehewa mbali na upendo wangu kwa ajili yenu" au "mmesamehewa kwa kwa faida yenu"

2 Corinthians 2:12

Sentensi unganishi

Paulo anawatia moyo wakristo katika Korintho kwa kuwaambia kuhusu fursa aliyokuwa nayo kuihubiri injili katika Troa na Makedonia.

Bwana alikuwa amenifungulia mlango ...kuihubiri Injili

Paulo anazungumza juu ya fursa yake ya kuhubiri injili kama ilivyokuwa mlango kupitia ambao alikuwa amekubaliwa kuupitia. " Bwana alimfungulia mlango ...kuhubri injili" au " Bwana alimpatia fursa ....kuhubiri injili"

Sikuwa na amani moyoni

"Moyo wangu ulifadhaishwa " au "Nilitiwa hofu"

ndugu yangu Timotheo

Paulo anazungumza kuhusu Timotheo kama kiongozi wake wa kiroho.

"Hivyo niliondoka"

"Hivyo niligana na watu wa Troa"

2 Corinthians 2:14

Mungu , ambaye ni Kristo daima hutuongoza katika ushindi

Paulo anazungumza kuhusu Mungu kama vile angekuwa askari mshindi anayeongoza jeshi na kwa yeye mwenyewe na watenda kazi pamoja naye kama wale wanaoshiriki katika jeshi lile. " Mungu, ambaye ni Kristo daima hutufanya sisi tushiriki katika ushindi au " Mungu, ambaye ni Kristo daima hutuongoza sisi katika ushindi kama vile wale walio juu yeye kama vile alivyopata ushindi"

Kupitia sisi husambaza harufu nzuri ya manukato ya maarifa yake kila mahali

"" Paulo anazungumza juu ya maarifa ya Kristo kama vile manukato yaliyo na harufu nzuri " "Huyafanya maarifa ya Kristo kuenea kwa kila mtu anayetusikia sisi, kama vile manukato mazuri ya ubani uliounguzwa humfikia kila mmoja aliye karibu"

kila mahali

kila mahali tuendako

kwa Mungu tu manukato mazuri ya kristo

Paulo anazungumza juu ya huduma yake ilikuwa kama sadaka ya kuteketezwa ambayo mtu fulani hutoa kwa Mungu.

manukato mazuri ya Kristo

"manukato mazuri ni maarifa ya Kristo" au "manukato mazuri ya ambayo Kristo hutoa"

wale waliookolewa

"wale ambao Mungu amewaokoa"

2 Corinthians 2:16

ni harufu

"maarifa ya Kristo ni manukato ."

harufu kutoka kifo hadi kifo

hili neno "kifo" limerudiwa kuweka msisitizo na tungo ina maanisha " harufu ya manukato inasababisha kifo" au "harufu ya manukato ya kifo ambayo husababisha wau kufa"

mmoja anayeokolewa

"mmoja ambaye kwake Mungu anamwokoa"

harufu ya manukato kutoka uhai hadi uhai

neno "uhai" limerudiwa kutoa msisitizo na tungo ina maanisha" harufu nzuri ya manukato inayotoa uhai" au " harufu nzuri ya maisha inayowafanya watu waishi"

nani anayestahili vitu hivi

"hakuna anayestahili vitu hivi"

usafi wa nia

"nia iliyo safi"

Tunazungumza katika Kristo

Tunazungumza kama watu waliounganishwa kwa Kristo" au " tunazungumza kwa mamlaka ya Kristo"

kama tulivyotumwa kutoka kwa Mungu

"kama watu ambao Mungu amewatuma"

mbele za uso wa Mungu

"tunazungumza mbele za uwepo wa Mungu"

2 Corinthians 3

2 Wakorintho 03 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Paulo anaendelea kujitetea. Paulo anaona Wakristo wa Korintho kama ushahidi wa kazi yake.

Dhana maalum katika sura hii

Sheria ya Musa

Paulo anakumbuka wakati Mungu alitoa amri kumi juu ya vibao vya mawe. Hii inawakilisha sheria ya Musa. Sheria ilikuwa nzuri kwa sababu ilitoka kwa Mungu. Lakini Mungu aliwaadhibu Waisraeli kwa sababu hawakuitii. Sura hii inaweza kuwa vigumu kwa watafsiri kuelewa ikiwa Agano la Kale bado halijatafsiriwa. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lawofmoses and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#covenant and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#reveal)

Mifano muhimu ya matamshi katika sura hii

Mifano

Paulo anatumia mifano nyingi katika sura hii kuelezea kweli ngumu za kirorho. Haijulikani kama hii inafanya mafundisho ya Paulo rahisi au vigumu zaidi kuelewa. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Hili ni agano sio la andiko bali la Roho."

Paulo anatofautisha agano la kale na agano jipya. Agano jipya sio mfumo wa sheria na kanuni. Hapa "Roho" labda inamaanisha Roho Mtakatifu. Inaweza pia kuelezea asili ya agano jipya kuwa ya kiroho.(See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#spirit)

<< | >>

2 Corinthians 3:1

Sentensi Unganishi

Paulo anawakumbusha kuwa hajisifu kwa vile anavyowaambia kuhusu kile alichokifanya kuhusu Kristo.

Tunaanza kujisifu wenyewe tena ?

" Hatujaanza kujisifu wenyewe tena"

hatuhitaji barua za utambulisho kwenu au kutoka kwenu, kama watu wengine, tunafanya hivyo?

"Kwa hakika hatuhitaji barua za uthibitisho kwenu au kutoka kwenu, kama watu wengine wanavyofanya"

Barua za uthibitisho

Hii ni barua mtu huandika kujitambulisha na kutoa uthibitisho wa mtu mwingine.

Ninyi wenyewe ni barua yetu ya utambulisho wetu

Ninyi wenyewe ni sawa na barua ya utambulisho wetu"

Imeandikwa ndani ya mioyoni mwetu

"ambayo Kristo ameiandika mioyoni mwetu"

imejulikana na kusomwa na watu wote

"ambayo watu wote wanaweza kuifahamu na kuisoma"

ninyi ni barua kutoka kwa Kristo

" ninyi ni barua ambayo Kristo ameiandika"

imetolewa na sisi

"ambayo tuliitoa"

Imeandikwa siyo kwa wino...katika vibao vya mioyo ya watu

Paulo anafafanua kwamba Wakorintho ni sawa na barua ya kiroho, siyo sawa na barua ambayo wanandamu huandika kwa vifaa vinavoonekana.

Imeandikwa si kwa wino...bali kwa roho wa Mungu anyeishi

"siyo barua ambayo watu huandika kwa wino, bali ni barua ambayo imeandikwa na Mungu anayeishi"

Haikuandikwa juu ya mbao za mawe, bali imeandikwa juu ya mbao za mioyo ya wanadamu

"siyo barua ambayo watu huchonga juu ya mbao za mawe bali ni barua ambayo Roho wa Mungu anayeishi ameiandika juu ya mbao za mioyo ya watu"

mbao za mioyo ya watu

Paulo anazungumza kuhusu mioyo yao ambayo imekuwa kama vipande bapa vya mawe au udongo wa mfinyanzi juu yake watu wamechora barua.

2 Corinthians 3:4

huu ndiyo ujasiri

Inaelezea kwa kile ambacho Paulo amekisema. .Ujasiri wake unatoka katika kufahamu kwamba Wakorintho ni uthibitisho wa huduma yake mbele za Mungu.

Uhodari ndani yetu wenyewe

"Kustahili kwetu ndani yetu sisi wenyewe" au "Utoshelevu ndani yetu sisi wenyewe"

kudai kitu chochote kuwa kinatoka kwetu

kudai kuwa kitu chochote ambacho tumefanya katika huduma huduma huja kwa juhudi zetu sisi wenyewe"

Uhodari wetu unatoka kwa Mungu

"Mungu hutupa utoshelevu"

Agano lisilo la barua

"agano ambalo halijajikita juu ya sheria ambazo zimeandikwa na wanandamu.

lakini la Roho

"lakini ni agano ambalo limejikita juu ya kile ambacho Roho anafanya"

barua inaua

"sheria iliyoandikwa hupelekea kifo"

2 Corinthians 3:7

Sentensi Unganishi

Paulo anatofautisha utukufu unaofifia wa patano la kale na ubora na uhuru wa patano jipya. Anatofautisha utando wa Musa na ubayana wa ufunuo wa sasa. Wakati wa Musa haukuwa picha ya wazi ya kile ambacho asa kimewekwa wazi.

Sasa huduma ambayo imeleta kifo ...ilikuja katika utukufu kama huo

Paulo anasisitiza kwamba ingawa sheria hupelekea huongoza katika kifo, Bado ilikujwa na ya utukufu mwingi.

huduma ambayo ilileta kifo

"huduma ambayo imesababisha kifo ka sababu imejikita juu ya sheria"

imechora katika barua juu ya mawe

"kwamba Mungu ameichonga kwenye mawe pamoja na barua"

Katika utukufu huo

"katika utukufu mwingi"

Hii ni kwa sababu

"wasingeweza kutazama kwa sababu"

ni kwa kiwango gani utukufu mwingi utakuwa huduma ambayo Roho huifanya?

Paulo anatumia swali hili kusisitiza kuwa "huduma ambayo Roho huitenda" ni lazima iwe ya utukufu kuliko "huduma ambayo ilitolewa" kwa sababu huongoza katika uzima "

huduma ambayo Roho huitenda

"huduma ya Roho." Hii inaelezea patano jipya, ambalo Paulo ni mtumishi wake.

2 Corinthians 3:9

kazi ya hukumu

"Kaziya hukumu ."Hii inarejea kwenye sheria ya Agano la Kale.

ni mara ngapi zaidi huduma ya haki huzidi sana katika utukufu!

Hapa neno "jinsi gani" linaonyesha tungo hii kama mshangao, siyo kama vile swali.

huduma ya uadilifu huzidi sana katika utukufu

Paulo anazungumza juu ya "huduma ya haki" kama ilivyokuwa taswira ammbayo ingeweza kutoa au kuongeza taswira nyingine. Anamaanisha kuwa " huduma ya uadilifu" ni ya utukufu zaidi kuliko sheria , ambayopia ilikuwa na utukufu.

huduma ya uadilifu

"huduma ya uadilifu" Inarejea kwenye agano jipya , ambalo paulo ni mtumishi wake.

kile kilichofanywa utukufu kwanza hakina utukufu tena katika heshima hii, kwa sababu ya utukufu unaozidi.

Sheria ya Agano la Kale haionekani tena kutukuzwa inapolinganishwa na Agano jipya, ambalo lina utukufu zaidi.

kile kilichofanywa utukufu kwanza

"kile kinachoweza kutafsiriwa katika kauli tendaji" "sheria ambayo Mungu aliifanya utukufu"

katika heshima hii

"kwa njia hii"

kile ambacho kilikuwa kinapita

IHii inamaanisha "huduma ya hukumu" ambayo Paulo anazungumza juu yake iliyokuwa kama taswira yenye uwezo wa kutoonekana.

2 Corinthians 3:12

Kwa kuwa tunaujasiri sana.

Hii ina maanisha kwamba Paulo tayari amesema. Ujasiri wake unatoka katika kufahamu kuwa agano jipya lina utukufu wa milele.

mwisho wa utukufu ambao ulikuwa unatoweka

Ni marejeo ya utukufu ambao ulinga'ra juu ya uso wa Musa kama ulivyofifia mbali kabisa.

2 Corinthians 3:14

Lakini fahamu zao zilikuwa zimefungwa

"Lakini mioyo yao ilikuwa migumu." Paulo anazungumza juu ya mioyo ya watu wa Israeli kama kifaa ambacho chaweza kufungwa au kufanywa kigumu. Ufafanuzi huu humaanisha kwamba walikuwa hawawezi kuelewa kile wanacho kiona.

Hata mpaka siku hii

Tungo hizi zinarejea akati ambao Paulo alikuwa akiandika kwa Wakorintho.

utaji uleule bado unabaki juu ya usomaji wa agano la kale

kama ilivyo kwa Waisraeli wasingeweza kuona utukufu juu ya uso wa Musa kwa sababu alifunika uso wake na utaji , kuna utaji wa kiroho unaowazuia watu kutoelewa wanaposema agano la kale.

juu ya usomaji wa agano la kale

"Wakati mtu anaposema agano la kale" au " Wakati wanaposikia mtu fulani anaposoma agano la kale"

Haijawekwa wazi, kwa sababu ni katika Kristo pekee inaondolewa mbali.

Hapa inajumuisha usahihi wa neno "hilo" inarejea "utaji uleule"

wakati wowote Musa asomwapo

Hapa neno " Musa" linarejea kwenye sheria ya agano la kale.

utaji hukaa juu ya mioyo yao

hapa neno "mioyo"linarejea kwenye moyo na mawazo. Utaji wa kiroho hufunika mioyo yao, kuwazuia wasiweze kuelewa agano la kale.

utaji unaondolewa.

Hii ina maanisha kwamba sasa wamepewa uwezo wa kufahamu.

2 Corinthians 3:17

Sasa sisi sote

Hapa neno "sisi" lina maanisha kwa wakristo wote, akiwemo na Paulona Wakorintho.

pamoja na nyuso zisizo wekewa utaji, huona utukufu wa Bwana

Sivyo kama Waisraeli amabao wasingeweza kuuona utukufu wa Mungu kwenye uso wa Musa kwa sababu alikuwa ameufunika kwa utaji, hakuna kitu chochote cha uwazuia waamini kuuona na kuufahamu utukufu wa Mungu.

Tunabadilishwa ndani ya muonekano uleule

Roho anawabadilisha waamini kuwa wenye utukufu kama yeye

kutoka shahada moja ya utukufu kwenda nyingine

"kutoka katika kipimo kimoja cha utukufu kwenda kwenye kipimo kingine cha utukufu.

kama ilivyo kutoka kwa Bwana

"kama vile ilivyo kutoka kwa Bwana"

2 Corinthians 4

2 Wakorintho 04 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Sura hii inaanza na neno "kwa hiyo." Neno hili linaunganisha na neno lililofundishwa katika sura ya awali. Jinsi sura hizi zinagawanyika inaweza kumchanganya msomaji.

Dhana maalum katika sura hii

Huduma

Paulo anawahudumia watu kwa kuwaambia kuhusu Kristo. Yeye hajaribu kuwadanganya watu kuamini. Ikiwa hawaelewi injili, ni kwa sababu tatizo ni la kiroho. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#spirit)

Mifanu muhimu ya matamshi katika sura hii

Mwanga na giza

Biblia mara nyingi inazungumza juu ya watu wasio na haki, watu ambao hawana fadhili za Mungu, kama wanaozunguka gizani. Inazungumzia mwanga ni kama inawawezesha watu wenye dhambi kuwa waadilifu, kuelewa kile wanachokosea na kuanza kumtii Mungu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous)

Maisha na kifo

Paulo hataji hapa maisha ya kimwili na kifo ya kimwili. Maisha inawakilisha maisha mapya Mkristo aliyo nayo katika Yesu. Kifo kinawakilisha njia ya zamani ya kuishi kabla ya kumwamini Yesu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#life and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#death and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Matumaini

Paulo anarudia katika mawazo kwa namuna ya kimakusudi. Anatoa taarifa. Kisha anatoa maneno yanayoonekana kuwa kukataa au kupinga au kutoa utofauti. Haya yote pamoja yanampa msomaji tumaini katika hali ngumu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#hope)

<< | >>

2 Corinthians 4:1

Sentensi Unganishi

Paulo anaandika kuwa yeye ni mwaminifu katika huduma yake kwa kumhubiri Kristo, siyo kujisifia yeye mwenyewe. Anaonyesha kifo na maisha ya Yesu kwa jinsi alivyoishi ili kwamba maisha yafanye kazi katika maisha ya wakorintho.

Tuna huduma hii

Hapa neno"sisi" linamwakilisha Paulo na watenda kazi wenzake, lakini sasa kwa Wakorintho kwa vile ambavyo Mungu anatuhudumia na anatuonyesha rehema kwa kutubadilisha sisi tuwe zaidi kama yeye.

na kama ambavyo tumeipokea rehema

Tungo hii inaeleza jinsi Paulo na watumishi wenzake wanayo huduma hii" "Ni zawadi ambayo Mungu ameitoa kwao kwa njia ya rehema yake."

tumekataa njia zote za aibu na zilizofichika.

Hii inamaainisha kwamba Paulo na watumishi wenzake walikatataa kufanya "vitu vinavyo aibisha na vilivyofichwa." Haina maana kwamba walikuwa wamevifanya vitu hivi huko nyuma.

njia zote za aibu na zilizofichika

neno "zilizofichika" hufafanua vitu ambavyo ni vya "kuaibisha"

Hatuishi kwa hila

"ishi kwa udanganyifu"

hatulitumii vibaya neno la Mungu

Tungo hii inatumia mawazo mawili yenye ukanusho kuelezea wazo chanya

tunajionyesha wenyewe kwa dhamiri ya kila mtu

Maana yake kwamba wanatoa ushahidi wakutosha kwa kila mtu anayewasikiliza kuamua ikiwa wako sahihi au hapana.

mbele ya Mungu.

Ina maanisha kwenye uwepo wa Mungu. Ufahamu wa Mungu na uthibitisho wa ukweli wa Paulo umetafsiriwa kama Mungu kuweza kuwaona.

2 Corinthians 4:3

Lakini kama injili yetu imefichika, imefichika kwa wale tu wanaoangamia

Hiki marejeo ya nyuma 3:14 mahali ambapo Paulo anaeleza kuwa kuna utaji wa kiroho amabao unawazuia watu wasielewe wakati wanaposoma agano la kale. Kwa njia hiyo, watu hawawezi kuifahamu injili.

Ikiwa injili yetu imetiwa utaji, imetiwa utaji

Hii inaweza kuelezwa katika muundo wa utendaji" ikiwa utaji unaifunika injili yetu, utaji huo huifunika"

Injili yetu

"Injili ambayo tunaihubiri"

mungu wa ulimwengu huu amewapofusha fahamu zao zisizoamini.

Paulo anazungumza juu ya mioyo yao ikiwa kama mioyo yao haiwezi kuona "mungu wa ulimwengu amewazuia wasioamini kuelewa"

mungu wa ulimwengu huu

"mungu anayetwala dunia," Tungo hii ina maanisha shetani.

hawawezi kuona nuru ya injili ya utukufu wa Kristo

Kama vile waisraeli walivyoshindwa kuuona utukufu wa Mungu uliong'ara juu ya uso wa Musa kwa sababu aliufunika kwa utaji.Wasio amini hawawezi kuuona utukufu wa Kristo unao ng'ara katika injili.

nuru ya injili

"nuru ambayo inakuja kutoka katika injili"

injili ya utukufu wa Kristo

"injili inayohusu utukufu wa Kristo"

2 Corinthians 4:5

Bali Kristo Yesu kama Bwana, na sisi wenyewe kama watumishi wenu

Unaweza ukaligawa tendo katika tungo hizi"Bali twamtangaza Kristo Yesu kuwa Bwana na tunatangaza sisi wenyewe kama watumishi wenu.

Kwa faida ya Kristo

"kwa sababu ya Yesu"

Nuru itang'aa toka gizani

Kwa sentensi hii, Paulo anarejea kwa Mungu kuumba nuru, kama ilivyoelezwa katika kitabu cha Mwanzo.

Ameangaza katika mioyo yetu, kutoa mwanga wa maarifa ya utukufu wa Mungu

Hapa neno "nuru" lina maanisha uwezo wa kuelewa.Kama vile Mungu alivyoumba nuru, yeye pia huumba ufahamu kwa waamini.

katika mioyo yetu

Hapa neno " mioyo" lina maanisha akili na mawazo

mwanga wa maarifa ya utukufu wa Mungu

"nuru , ambayo ni maarifa ya utukufu wa Mungu"

utukufu wa Mungu katika uwepo wa Yesu Kristo.

"utukufu wa Mungu katika uso wa Yesu Kristo."

2 Corinthians 4:7

Lakini tuna

Hapa neno "tuna" lina maanisha Paulo na watenda kazi pamoja naye, lakini siyo kwa Wakorintho.

tuna hazina hii katika vyombo vya udongo

Paulo anazungumzia injili ilivyokua kama hazina na miili yao ilivyokuwa kama chupa za udongo zinazoweza kuvunjika. Hii inasisitiza kuwa wana thamani ndogo ukilinganisha na thamani ya injili ambayo wanaihubiri.

ili kwamba ieleweke

" ya kwamba iko dhahiri kwa watu" au "ya kwamba watu wanatambua wazi wazi"

Tunataabika katika kila hali

Hiki kinaweza kuelezwa katika kauli tendaji. "Watu hututaabisha kwa njia mbali mbali"

Tunateswa lakini hatujatelekezwa

. " Watu hututesa lakini Mungu hajatutelelkeza"

Twatupwa chini lakini hatuangamizwi

hututupa chini lakini hawatuangamizi"

Twatupwa chini

"twaumizwa vibaya"

iku zote tunabeba katika mwili wetu kifo cha Yesu

Paulo anazungumza juu ya mateso yake kuwa kama vile ni uzoefu wa kifo cha Yesu Kristo.

uzima wa Yesu uonekane pia katika miili yetu.

Maana zaweza kuwa "miili yetu itaishi tena, kwa sababu Yesu yu hai au " maisha ya kiroho ambaye Yesu hutoa pia yaonekane katika miili yetu."

uzima wa Yesu uonekane pia katika miili yetu.

Yaweza kueleza katika kauli tendaji " watu wengine wanaweza kuyaona maisha ya Yesu katika miili yetu"

2 Corinthians 4:11

Sisi tulio hai siku zote tumetolewa kufa kwa ajili ya Yesu

Kubeba kifo cha Yesu huwakilisha kuwa katika hatari ya kufa kwa sababu ya kuwa mwaminifu kwa Yesu.

ili kwamba uhai wa Yesu uonekane katika miili yetu ya kibinadamu

Mungu anahitaji maisha ya Yesu yaonekane kwetu. Maana pendekezwa zaweza kuwa "miili yetu itaishi tena, kwa sababu Yesu yu hai. au "maisha ya kiroho ambayo Yesu hutoa pia yaweza kuonyeshwa katika miili yetu"

ili kwamba uhai wa Yesu uonekane katika miili yetu ya kibinadamu

Sentensi hii inaweza kuelezwa katika kauli tendaji. "ya kwamba watu wengine wanan weza kuyaona maisha ya Yesu katika miili yetu"

kifo kinafanya kazi ndani yetu, bali uzima unafanya kazi ndani yenu.

Paulo anazungumzia kifo na uzima kama watu ambao wanaweza kufanyakazi. Hii ina maana kwamba daima wako katika hatari ya kifo cha mwili kwa hiyo Wakorintho wapate uzima wa kiroho.

2 Corinthians 4:13

roho ileile ya imani

'nia ileile ya imani"Hapa neno" roho" linamaanisha nia ya mtu na silika.

kulingana na kile kilicho andikwa

Sentensi hii inaweza kuelezwa katika kauli tendaji." kama mmoja yule anayeandika maneno haya"

Niliamini, na hivyo nilinena

Hii ni rejea ktoka katika kitabu cha Zaburi.

yule aliye mfufua Bwana Yesu pia atatufufua sisi pamoja naye

Neno "yuleyule"linamaanisha Mungu"

atatufufua sisi pamoja naye

Neno "sisi" linawatenga Wakorintho.

Kila kitu ni kwa ajili yenu

Neno "kila kitu" linamaanisha mateso yote ambayo Paulo aliyoyaelelza katika mistari iliyotangulia.

neema inavyo enea kwa watu wengi

Sentensi hii inaweza kuelezwa kwa jinsi hii "kama Mungu anavyoeneza neema yake kwa watu wengi"

shukurani zizidi kuongezeka

Paulo anazungumzia shukrani kuwa kama kitu ambacho kingekuja kuwa kikubwa kwa chenyewe.

2 Corinthians 4:16

Sentensi Unganishi

Paulo anaandika kwamba changamoto za Wakorintho ni ndogo na hazitadumu wakati zikilinganishwa na vitu vya milele visivyoonekana.

Hivyo hatukati tamaa

"Sentensi hii inaweza kuelezwa kwa jinsi hii" hivyo tunabakia wajasiri"

kwa nje tunachakaa,

Hii ina maanisha miili yao inaharibika na kufa.

kwa ndani tunafanywa upya siku hadi siku.

Ina maanisha utu wao wa ndani, kiroho maisha yanazidi kuimarika.

Kwa kipindi hiki kifupi, mateso haya mepesi yanatuandaa sisi kwa ajili ya umilele mzito wa utukufu

Paulo anazungumzia mateso yake na utukufu ambaoMungu atampa kuwa vilikuwa vitu vinavyoweza kupimika.

uzidio vipimo vyote

Utukufu wa uzoefu ambao Paulo ataupata ni mzito sana ambao hakuna awezaje kuupima.

Vitu tunavyoweza kuviona ni vya muda tu, bali vitu ambayo havionekani

Sentensi hii inaweza kuelezwa kwa jinsi hii. " vitu ambavyo twaweza kuviona...vitu ambavyo hatuwezi kuviona"

bali kwa ajili ya vitu visivyoonekana

Unaweza kuligawa tendo kwa tungo hizi. "lakini twangojea vitu ambavyo havionekani"

2 Corinthians 5

2 Wakorintho 05 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Miili mipya mbinguni

Paulo anajua kwamba atakapokufa atapata mwili bora zaidi. Kwa sababu hii, yeye haogopi kuuawa kwa ajili ya kuhubiri injili. Kwa hiyo anawaambia wengine kwamba wao pia wanaweza kuunganishwa na Mungu. Kristo ataondoa dhambi zao na kuwapa haki yake. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#goodnews, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#reconcile and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous)

Uumbaji mpya

Uumbaji wa zamani na uumbaji mpya unaelezea jinsi Paulo anavyoonyesha Uumbaji wa zamani na uumbaji mpya. Dhana hizi pia ni sawa na mtu wa zamani na mtu mpya. Neno "zamani" labda halielezei asili ya dhambi ambayo mtu anazaliwa nayo. Inamaanisha njia ya zamani ya kuishi au Mkristo aliyekuwa amefungwa katika dhambi. "Uumbaji mpya" ni asili mpya au maisha mapya ambayo Mungu humpa mtu baada ya kumwamini Kristo. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith)

Mfano muhimu ya matamshi katika sura hii

Nyumbani

Nyumbani mwa Wakristo haipo tena ulimwenguni. Nyumbani halisi mwa Mkristo iko mbinguni. Kwa kutumia mfano huu, Paulo anasisitiza kuwa mazingira ya Kikristo katika ulimwengu huu ni ya muda mfupi. Inatoa tumaini kwa wale wanaosumbuliwa. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#heaven and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#hope)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Ujumbe wa upatanisho"

Hii inahusu injili. Paulo anawaita watu ambao wana chuki kwa Mungu kutubu na kuunganishwa naye. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#repent and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#reconcile)

<< | >>

2 Corinthians 5:1

Sentensi Unganishi

Paulo anazidi kuitofautisha miili ya duniani ya waamini na ile ya mbinguni ambayo Mungu atawapa.

kam maskani ya ulimwenguni ambayo tunaishi humo yanaharibiwa, tunalo jengo kutoka kwa Mungu.

Paulo anazungumzia mwili wake unaoonekana ni kama ulikuwa wa muda "makao ya duniani" na ya ufufuo wa mwili Mungu atatoa kama vile miili ya kudumu " jengo"

Ni nyumba isiyotengenezwa kwa mikono ya wanadamu

Hii ina maanisha " jengo kutoka kwa Mungu" Hii inaweza kuelezwa ka jinsi hii. " ni nyumba ambayo haikutengenezwa na wanandamu"

katika hema hii tunaugua

Neno "hema" linaelezea " makao ya duniani ambayo tunaishi." Neno tunaugua ni sauti ya mtu anayoitoa pindi wanapokuwa wanatamani kuwa na kitu fulani ambacho ni kizuri.

tukitamani kuvikwa kwa maskani yetu mbinguni

Maneno " makao yetu ya mbinguni" yana maanisha "jengo kutoka kwa Mungu." Paulo anazungumzia ufufuo wa mwili kama vile ulikuwa pamoja jengo na kipande cha nguo ambacho mtu anaweza kuvaa.

kwa kuivaa

"kwa kuivaa makao yetu ya mbinguni"

hatutaonekana kuwa tu uchi.

Hii inaweza kuelezwa kwa jinsi hii: "hatutakuwa uchi" au "Mungu hatatukuta tukiwa uchi"

2 Corinthians 5:4

tuko ndani ya hema hii

Paulo anazungumzia mwili unaoonekana kama vile ulikuwa "hema."

ndani ya hema hii, twaugua tukilemewa

Neno " hema" linamaanisha makao ya duniani ambayo tunaishi ndani yake." Neno " ugua" ni sauti anayoitoa mtu wakati wanapohitaji kutamani kuwa na kitu ambacho ni kizuri.

tukilemewa

Paulo anarejea kwenye changamoto ambazo mwili hupitia kama vile zilikuwa vitu ambavyo ni vizito kuvibeba.

Hatutaki kuvuliwa badala yake, tunataka kuvalishwa

Paulo anazungumzia mwili kama vile ulikuwa umevikwa.Hapa "kuvuliwa" lina maanisha kifo ccha mwili; " kuvalishwa" lina maanisha kuwa na ufufuo wa mwili ambao Mungu atautoa.

kuvuliwa

"kutokuwa na nguo" au "kuwa uchi"

ili kwamba kile kilicho kufa kiweze kumezwa na uzima

Paulo anazungumzia maisha kama vile yalikuwa mnyama ambaye hula " ambaye hufa." Mwiliunaoonekana ambaomutakufa utahuishwa kwa njia ya ufufuo wa mwili ambao utaishi milele.

ili kwamba kile kilicho kufa kiweze kumezwa na uzima

Hii inaweza kusemwa kwa jinsi hii: "ili kwamba uhai utaki meza kile ambacho ni cha kufa"

ambaye alitupa sisi Roho kama ahadi ya kile kitakacho kuja.

Roho anayezungumzwa alikuwa kama malipo ya chini ya muda kuhusu uzima wa milele.

2 Corinthians 5:6

Sentensi Unganishi

Kwa sababu waamini watakuwa na miili mipya na kuwa na Roho Mtakatifu kama ahadi, Paulo anawakumbusha kuishi kwa imani ili waweze kumfurahisha Bwana. Anaendelea kuwakumbusha kuwavuta na wengine kwa sababu waamini wataonekana katika kiti cha hukumu cha Kristo na kwa sababu ya pendo la Kristo aliyekufa kwa ajili ya waamini.

wakati tuko nyumbani katika mwili

Paulo anazungumza juu ya miili inayoonekana kama vile ilikuwa mahali ambapo mtu hukaa.

tuko mbali na Bwana.

"hatuko nyumbani pamoja na Bwana " au " hatuko mbinguni pamoja na Bwana"

tunatembea kwa imani, sio kwa kuona

"tunaishi kwa imani, na siyo kwa mujibu wa kile tunachokiona"

Ni bora tuwe mbali kutoka kwenye mwili

Hapa neno "mwili" lina maanisha "mwili unaoonekana"

nyumbani pamoja na Bwana.

"nyumbani pamoja na Bwana mbinguni"

2 Corinthians 5:9

tukiwa nyumbani au mbali

Neno " Bwana" huenda limetokana na mistari iliyotangulia. " ikiwa tukiwa numbani pamoja na Bwana au mbali na Bwana"

tumpendeze yeye

"kumpendeza Bwana"

mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo

"mbele za Kristo kuhukumiwa"

kila mmoja aweze kupokea kile kinachostahili

"kilamtu aweze kupokea kile anacholstahili"

mambo yaliyotendwa katika mwili

Sentensi yaweza kuelezwa kwa jinsi hii: "vitu ambavyo amevifanya katika mwili unaoonekana"

ikiwa ni kwa uzuri au kwa ubaya.

"ikiwa vitu hivyo vilikuwa vizuri au vibaya"

2 Corinthians 5:11

kuijua hofu ya Bwana

"kuijua nini maana ya kumhofu Mungu"

Jinsi tulivyo, inaonekana wazi na Mungu

Sentensi hii inaweza kuelezwa kwa jinsi hii: "Mungu hutuona dhahiri wanadamu jinsi tulivyo"

hivyo mnaweza kuwa na majibu

"hivyo mnaweza kuwa na kitu cha kusema juu yake"

inaeleweka pia kwenye dhamiri zenu

"kwamba pia mmedhihirishwa kwayo"

ili kwamba muweze kuwa na jibu

"ili kwamba muweze kuwa na kitu cha kusema"

wale wanaojivunia kuhusu mwonekano lakini sio kile kilicho ndani ya moyo

Katika sentesi hii Neno "kuonekana" linaelezea mwonekano wa nje wa vitu kama vile uwezo, na hali.Neno "moyo" lina maanisha utu wa tabia ya ndani ya mtu.

2 Corinthians 5:13

ikiwa kama tumerukwa na akili

Paulo anazungumza kuhusu namna wengine wanavyomfikiria yeyey na watenda kazi pamoja naye.

Pendo la Kristo

Maana zinazowezekana ni: "Upendo wetu kwa Krist" au Pendeo la Kristo kwetu."

alikufa kwa ajili ya wote

"alikufa kwa ajili ya watu wote"

yeye mwenyewe alikufa na alifufuka

Katika sentensi hii neno " yeye" linamaanisha "Kristo"

2 Corinthians 5:16

Sentensi Unganishi

Kutokana na pendo la Kristo, na kifo chake, hatupaswi kuhukumu kwa vigezo vya kibinadamu.Tumechaguliwa kuwafundisha wengine jinsi ya kuungamanishwa pamoja na kuwa na amani pamoja na Mungu kwa njia ya kifo cha Kristo na kupokea uadilifu kwa njia ya Kristo.

Kwa sababu hii

Ina maanisha kile ambacho Paujlo amekisema kuhusu kuishi kwa ajili ya Kristo badala ya kuishi kwa ajili ya nafsi.

yeye ni kiumbe kipya.

Paulo anazungumza juu ya mtu anyeamini katika Kristo kama vile ameumba mtu mpya

Mambo ya kale yamepit

"mambo ya kale" ina maanisha vitu vinavyoelezea tabia ya mtu kabla ya kumwamini Yesu Kristo.

2 Corinthians 5:18

vitu vyote

"Mungu amefanya vitu hivi vyote." Ina maanishna kile ambacho Paulo alikisema katika mistari iliyotangulia kuhusu vitu vipya kushika nafasi ya vitu vya kale.

huduma ya upatanisho

Yaweza kutasiriwa na tungo tendo " huduma ya kuwapatanisha watu kwake"

Hiyo ni kusema

"hii ina maansha"

katika Kristo, Mungu anaupatanisha ulimwengu kwake mwenyewe

Katika sentensi hii neno" ulimwengu" lina maana ya watu walionmo duniani.

Anawekeza kwetu ujumbe wa upatanisho

Mungu amempa Paulo wajibu wa kueneza ujumbe kwamba Mungu anawapatanisha watu kwa yeye.

Ujumbe wa upatanisho

"ujumbe kuhusu uapatanisho"

2 Corinthians 5:20

tunateuliwa kama wawakilishi wa Kristo,

Sentensi hiiyaweza kuelezwa kwa jinsi hii: " Mungu ametuchagua kama wawakilishi wa Kristo.

wawakilishi wa Kristo

"wale waanao mhubiri Kristo

Mpatanishwe kwa Mungu

Ina maanisha "Mungu na awapatanishe kwake"

Alimfanya Kristo kuwa sadaka kwa ajili ya dhambi zetu

"Mungu alimfanya Kristo kuwa sadaka kwa ajili ya dhambi zetu"

dhambi zetu...ili tuweze kufanyika

Neno "yetu" na "sisi" tumejumuishwa na inamaanisha waamini wote.

Yeye ndiye ambaye hakutenda dhambi

"Kristo ni yeye pekee ambaye hakuwahi kutenda dhambi"

Alifanya hivi ili tuweze kufanyika haki ya Mungu katika yeye

"Mungu alifanya hivi ili tuweze kufanyika haki ya Mungu kaika Kristo"

li tuweze kufanyika haki ya Mungu katika yeye.

Tungo "haki ya Mungu" inamaanisha haki ambayo Munguanaihitaji na ambayo inatoka kwa Mungu.

2 Corinthians 6

2 Wakorintho 06 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri huweka kila mstari wa mashairi upande wa kulia zaidi kuliko maandiko yote ili iwe rahisi kusoma. ULB inafanya hivi kwa mistari 2 na 16-18, ambayo ni maneno kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

Watumishi

Paulo anawakilisha Wakristo kama watumishi wa Mungu. Mungu anawaita Wakristo kumtumikia katika hali zote. Paulo anaelezea baadhi ya hali ngumu ambako yeye na wenzake walimtumikia Mungu.

Mfano muhimu ya matamshi katika sura hii

Maneno ya tofauti

Paulo anatumia jozi nne za utofauti: haki dhidi ya uasi, mwanga dhidi ya giza, Kristo dhidi ya Shetani, na hekalu la Mungu dhidi ya sanamu. Tofauti hizi zinaonyesha tofauti kati ya Wakristo na wasio Wakristo. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#light and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#darkness)

Mwanga na giza

Biblia mara nyingi inazungumzia watu wasio na haki, watu ambao hawampendezi Mungu, kama kwamba walikuwa wakizunguka gizani. Inazungumza juu ya mwanga ni kama inawawezesha watu wenye dhambi kuwa waadilifu, na kuelewa kile wanachokosea na kuanza kumtii Mungu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous)

Maswali ya uhuishaji

Paulo anatumia maswali ya uhuishaji mfululizo kwa kufundisha wasomaji wake. Maswali haya yote yana maana sawa sawa: Wakristo hawapaswi kushirikiana na wale wanaoishi katika dhambi. Paulo anarudia katika maswali haya kwa msisitizo. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-rquestion and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Sisi

Labda Paulo anatumia neno "sisi" kuwakilisha Timotheo na yeye mwenyewe. Au labda anawajumuisha watu wengine pia.

<< | >>

2 Corinthians 6:1

Sentensi Unganishi

Paulo anajumuisha jinsi gani kufanya kazi kwa pamoja inavyopaswa kuwa.

Habari za Jumla

Katika mstari wa pili Paulo an nukuu kifungu kutoka kwa nabii Isaya.

Kufanya kazi Pamoja

Paulo anamaanisha kuwa yeye na Timotheo wanatumika pamoja na Mungu

tunawasihi ninyi msiipokee neema ya Mungu pasipo matokeo

Paulo anawasihi paoja nao kuiruhusu neema ya Mungu kufanya kazi katika maisha yao.

Kwa kuwa anasema

"Kwa kuwa Mugu anasema" Hii inatambulisha nukuu kutoka kwa nabii Isaya. "Kwa kuwa Mungu anasema katika maandiko"

Tazama

Neno "Tazama" mahali hapa linatukumbusha kuwa wasikivu kwa habari zijazo zinazostajabisha.

Hatuweki jiwe la kizuizi mbele ya mtu yeyote,

Paulo anazungumzia juu ya kitu chochote ambacho kinaweza kumzuia mtu kutotumaini katika Kristo kama vile ilivyokuwa kifaa cha mwili juu ya kile ambacho mtu yule huteleza na kuanguka.

kwa kuwa hatuitakii huduma yetu iletwe katika sifa mbaya.

Neno "sifa mbaya " lina maanisha watu kusema vibaya kuhusu huduma ya Paulo .

2 Corinthians 6:4

Habari za Jumla

Wakati Paulo anapotumia neno " sisi", ana maanisha yeye mwenyewe na Timotheo.

Tunajihakiki wenyewe kwa matendo yetu yote, kwamba tu watumishi wa Mungu.

"Tunathibitisha kjwa sisi ni watumishi wa Mungu kwa kila kile tulifanyalo"

Tu watumishi wake katika wingi wa ustahimilivu.... katika kukosa usingizi usiku, katika njaa

Paulo anataja maeneo mbali mbali ya mazingira magumu katika hayo wanathibitisha kuwa ni watumishi wa Mungu.

katika usafi...katika upendo halisi.

Paulo anaorodhesha mambo mbalimbali ya uadilifu ambayo waliyatunza wakati wa mazingira magumu na inathibisha kuwa ni watumishi wa Mungu.

Tu watumishi wake katika neno la kweli, katika nguvu ya Mungu

Kuwekwwakfu kwao kuihubiri injili katika nguvu za Mungu inathibitisha kuwa ni watumishi wa Mungu.

katika neno la kweli

"katika kuhubiri neno la kweli la Mungu"

Tuna silaha ya haki kwa ajili ya mkono wa kuume na wa kushoto

Paulo anazungumza juu ya uadilifu wao kama vile silama wanazozitumia kupigana vita vya kiroho.

Tuna silaha ya haki kwa ajili ya mkono wa kuuume na wa kushoto.

"uadilifu kama silaha yetu " au "uadilifu kama silaha zetu"

kwa mkono wa kuume na wa kushoto

Maana zaweza kuwa hizi: "kuwa kuna silaha katika mkono mmoja na ngao mkono mwingine" au "wamewezeshwa kikamilifu kwa vita , tayari kujilinda na mashambulizi kutoka sehemu yoyote."

2 Corinthians 6:8

Habari za Jumla

Paulo anaorodhesha mitazamo mingi jinsi watu wanavyofikiri juu yake na huduma yake.

Tunatuhumiwa kuwa wadanganyifu

Sentensi hii inaweza kuelezwa kwa jinsi hii: "watu hutushtaki kwa kuwa wadanganyifu"

kana kwamba hatujulikani na bado tunajulikana vizuri.

Sentensi hii inaweza kuelezwa kwa jinsi hii: "ikiwa kama watu hawakututambua sisi na bado watu wanatutambua vizuri"

Tazama!

Neno "Tazama" linatukumbusha kusikiliza kwa makini habari za kushangaza zinazofuata.

Tunafanya kazi kama tunaoadhibiwa kwa ajili ya matendo yetu lakini sio kama vile waliohukumiwa hata kufa.

Sentensi hii inaweza kuelezwa hivi": "tunatemda kazi kama vile watu wanatuadhibu kwa matendo yetulakini siyo kama vile wametuhukumu kufa"

2 Corinthians 6:11

Sentensi Unganishi

Paulo anawatia moyo waamini wa Korintho kujitenga na miungu naa kuishi maisha kwa ajili ya Mungu.

Tumezungumza ukweli wote kwenu,

"tumezungumza ukweli kwenu"

mioyo yetu imefunguka kwa upana.

paulo anazungumza alivyowaathiri Wakorintho kwa kuwa na moyo uliofunguka.

mioyo yenu haizuiliwi na sisi, bali mnazuiliwa na hisia

Paulo anazungumzia Wakorintho kwa kukosa upendo kwake kama vile mioyo yao ilikuwa imesongwa katika nafasi finyi.

mioyo yenu haizuiliwi na sisi,

Sentensi hi yaweza kuelezwa kwa jinsi hii: " Hatujaizuia mioyo yenu" au " hatujawapa mioyo yenu sababu yoyote kuacha kutupenda sisi"

mnazuiliwa na hisia zenu wenyewe

Sentensi hii yaweza kuelezwa katika hali tendaji: " hisia zenu zinawazuia " au : mmeacha kutupenda sisi kwa sababu zenu"

katika kubadilishana kwa haki

"kama mwitikio halisi

ninaongea kama kwa watoto

Paulo anawaeleza Wakorintho kama watoto wake w kiroho.

fungueni mioyo yenu kwa upana.

Paulo anawasihi Wakorintho kumpenda yeye kama yee alivyowapenda wao.

2 Corinthians 6:14

Habari za Jumla

Katika mstari wa 16, Paulo anachukua wazo la vifungu vingi kutoka manabii wa Agano la Kale "Musa, Zekaria, Amosi, na huenda na wengine.

Msifungamanishwe pamoja na wasioamini

Sentensi hii aweza kuelezwa kwa jinsi ya kukubali: "mfungamanishwe pamoja na waaamini peke yake"

lakini mfungamanishwe pamoja na

Paulo anazungumzia juu ya kufanya kazi pamoja kuelekea kusudi la pamoja kama vile ilivyo kwa wanyama wawili waliofungwa pamoja kuvuta jembe au mkokoteni.

kuna uhusiano gani kati ya haki na uasi?

Hili ni swali la kujihoji ambalo hutegemea jibu hasi.

Na kuna ushirika gani kati ya nuru na giza?

Paulo anauliza swali hili kusisitiza kuwa nuru na giza haviwezi kuchangamana maana nuru huondoa giza. Maneno "nuru" na "giza"? yanaelezea uboro wa maadili ya mwili na kiroho kwa waamini na wasioamini.

Ni makubaliano gani Kristo anaweza kuwa nayo na Beliari?

Hili ni swali la kujihoji ambalo linategemea jibu hasi.

Beliari

Hili ni jina jingine la mwovu.

Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na asiyeamini?

Sentensi hii aweza kuelezwa kwa jinsi ya kukubali: "mfungamanishwe pamoja na wasamini peke yake"

Na kuna makubaliano gani yapo kati ya hekalu la Mungu na sanamu?

Hili ni swali la kujihoji ambalo linategemea jibu hasi.

sisi ni hekalu la Mungu aliye hai

Paulo ana anamaanisha wakristo wote kuwa wanatengeneza hekalu ili Mungu kuishi ndani yake.

2 Corinthians 6:17

Habari za Jumla

paulo ananukuu sehemu kutoka manabii wa Agano la Kale, Isaya na Ezekeieli.

mkatengwe

Sentensi hii yaweza kuelezwa katika kauli tendaji: " mkajitenge" au " mniruhusu mimi niwatenge"

Msiguse kitu kichafu,

Sentensi hii yaweza kuelezwa kwa namna ya kukubali: "Gusa vitu ambavyo ni visafi pekee"

2 Corinthians 7

2 Wakorintho 07 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Katika mistari ya 2-4, Paulo anamaliza kujitetea kwake. Halafu anaandika juu ya kurudi kwa Tito na faraja iliyoletwa.

Dhana maalum katika sura hii

Usafi na uchafu

Wakristo ni "wasafi" kwa maana kwamba Mungu amewatakasa kutoka kwa dhambi. Hawakuhitaji ya kuwa na wasiwasi ya kuwa safi kulingana na sheria ya Musa. Kuishi kwa ukafiri huweza kumfanya Mkristo kutokuwa msafi. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#clean and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lawofmoses)

Huzuni na masikitiko

Maneno "huzuni" na "masikitiko" katika sura hii yanaonyesha kwamba Wakorintho walikuwa wamesononeka kiasi cha kutubu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#repent)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Sisi

Labda Paulo anatumia neno "sisi" kuwakilisha Timotheo na yeye mwenyewe. Au labda anawajumuisha watu wengine pia.

Hali ya awali

Sura hii inazungumzia kwa kina hali nyingine ya awali. Tunaweza kufikiria mambo fulani ya hali hii kutokana na taarifa katika sura hii. Lakini ni bora kutoingiza aina hii ya habari kamili katika tafsiri. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

<< | >>

2 Corinthians 7:1

Sentensi Unganishi

Paulo anaendelea kuwakumbusha wao kujitenga na dhambi na kutafuta utakatifu kwa makusudi.

Wapendwa wangu

"ninyi niwapendao" au rafiki wapenzi"

na tujitakase wenyewe

Katika sentensi hii Paulo anasema kujitenga mbali na dhambi ambayo yaweza kuathiri uhusiano wa kila mtu na Mungu.

Na tuutafute utakatifu

"na tujitahidi kuwa watakatifu"

katika hofu ya Mungu

"katika hofu ya ndani kwa Mungu"

2 Corinthians 7:2

Sentensi Unganishi

Akiwa tayri amewaonya watu wa Korintho kuhusu viongozi wengine ambao walikuwa wakijitahidi kuwavuta Wakorintho wawafuate wao, lakini Paulo anawakumbusha watu jinsi anavyowafikiria.

Fanyeni nafasi kwa ajili yetu

Inarejea kile ambacho Paulo alikisema awalikatika 6:11 kuhusu wao kufungua mioyo yao kwa yeye.

Siyo kuwahukumu ninyi kuwa nasema hili

"sisema hili kuwashitaki ninyi kwa kufanya vibaya." Neno "hili" linarejea kwa kila ambacho Paulo alikuwa amesema kuhusu ambavyo hakumkosea mtu yeyote.

mmo mioyoni mwetu

Paulo anazungumza kwa ajili yake na pendo kuu la washirika wake kwa ajili ya wakorintho kama vile wamefanyika ndani ya kioyo yao.

kwetu sisi kufa pamoja na kuishi pamoja

Hii ina maanisha kwamba Paulo na washirika wake wataendelea kuwapenda Wakorintho bila kujali kinachotokea.

kwetu sisi kufa

"sisi" inajumuisha waamini wa Korintho"

Nimejawa na faraja

Yaweza kuelezwa katika jinsi ya utendaji: : "Mnanijaza faraja"

Ninajawa na furaha

Pulo anazumzia furaha kama vile kimiminika ambacho humjaza yeye mpaka anajawa.

hata katikati ya mateso yetu yote.

"licha ya taabu zetu"

2 Corinthians 7:5

Tulikuja Makedonia

Neno "sisi"lina maanisha Paulo na Timotheo na siyo Wakorintho au Tito.

miili yetu haikuwa na pumzikO

neno "miili"linaelezea utu wote wa mwanadamu

Tulipata taabu kwa namna zote

Hii yaweza kuelezwa kwa jinsi ya utendaji: " tulipitia mateso katika kila njia"

tulipata taabu kwa namna zote kwa kupigwa vita upande wa nje na hofu upande wa ndani

Maana zinazopendekezwa kwa neno" nje" "ni nje ya miili yetu" au "nje ya kanisa." Neno "ndani" linaelezea hisia zao za ndani.

kwa faraja zile Tito alizopokea kutoka kwenu

Paulo alipokea faraja kwa katika kutambua kuwa Wakorintho walikuwa wamemfariji Tito

2 Corinthians 7:8

Sentensi Unganishi

Paulo anawasifu kwa huzuni yao ya ucha mungu, ari yao ya kutenda haki, na furaha ambayo ilimleta yeye na Tito.

Habari za Jumla:

Hii inarejea kwenye barua ya kwanza ya Paulo kwa hawa waamini wa Wakorintho ambapo aliwakemea wakristo kukubali mtu kufanya zinaa na mke wa baba yake.

wakati nilipoona waraka wangu

"wakati nilipojifunza waraka wangu"

si kwa sababu mlikuwa na shida

Sentensi hii yaweza kuelezwa kwa jinsi ya utendaji"siyokwa sababu kile nilichokisema katika barua yangu kiliwahizunisha ninyi"

mliteseka si kwa hasara kwa sababu yetu

"mliteseka si kwa hasara kwa sababu tuliwakemea" Hii ina maa kuwa barua hiyo iliwasababishia huzuni, haukupita muda mrefu walifaidika kutokana na barua ile kwa sababu iliwaongoza kwenye toba

Kwa kuwa huzuni ya kiungu huleta toba ambayo hukamilisha wokovu

Neno "toba" laweza kurudiwa kufafafnua uhusiano wake kwa kile kilichotangulia na kile kinachofuata.

bila kujuta

Maana zaweza kuwa " Paulo hajuti kwamba amewasababishia huzuni kwa sababu huzuni hiyo iliwaongoza kwenye toba na wokovu) au Wakorintho hawatajuta kupitia huzuni kwa sababu inawaongoza kwenye toba yao na wokovu.

Huzuni ya kidunia, hata hivyo, huleta mauti

Aina hii ya huzuni hupelekea kifo badala ya wokovu kwa sababu haileti toba

2 Corinthians 7:11

Angalieni

Neno hililinaweka msisitizo kwa kile kitakachozungumzwa baadaye.

Jinsi gani azma ilikuwa kubwa ndani yenu kuthibitisha kuwa hamkuwa na hatia

Neno " jinsi gani" linaifanya sentensi hii kuwa mshangao.

uchungu wenu

"hasira yenu"

kwamba haki inapaswa kutendeka

Yaweza kuelezwa kuwa: "mtu yule anapaswa kubeba uadilifu.

mkosaji

"yule aliyetenda mabaya"

ili kwamba udhati wa mioyo yenu kwa ajili yetu ifanywe kujulikana kwenu

Sentensi hii yaweza kuelezwa kwa kauli tendaji kuwa: kwamba mmekuwa na udhati wa mioyo yenu kwa ajili yetu katika unyoofu.

mbele ya macho ya Mung

Hii inarejea kwenye uwepo wa Mungu na uthibitisho wa uaminifu wa Paulo umemaanishwa kama Mungu amekua aliwaona wao.

2 Corinthians 7:13

Ni kwa ajili ya hii kwamba tunafarijika

Hapa neno "hii" lina maanisha jinsi ambsvyo Wakorintho waliitikia kwa barua ya kwanza ya Paulo, kama alivyoeleza katika mistari ya mwanzo.

roho yake iliburudishwa na ninyi nyote

Hapa neno "roho" linaelezea silika ya mtu na mioyo yao .

Kwa kuwa kama nilijivuna kwake kuhusiana na ninyi

"kama ikiwa nilijivuna kwake kuhusu ninyi"

sikuwa na aibu

"hamkunikatisha tamaa"

Majivuno yetu kuhusu ninyi kwa Tito yalithibitisha kuwa kweli.

"ninyi mlithibitisha kuwa kujivuna kwetu kuhusu ninyi na Tito kulikuwa kweli."

2 Corinthians 7:15

utii wenu ninyi nyote

Hili jina "utii" linaweza kuelezwa pamoja na tendo "tii".

mlivyomkaribisha kwa hofu na kutetemeka

Neno "hofu" na "kutetemeka"hueleza maana ileile na kusisitiza ongezeko la hofu.

kwa hofu na kutetemeka.

Maana zaweza kuwa )" kwa hofu kubwa kwa Mungu ) au kwa hofu kubwa kwa Tito.

2 Corinthians 8

2 Wakorintho 08 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Sura za 8 na 9 zinaanza sehemu mpya. Paulo anaandika kuhusu jinsi makanisa ya Ugiriki yalivyowasaidia waumini maskini huko Yerusalemu.

Baadhi ya tafsiri huweka nukuu kutoka kwenye Agano la Kale kwa upande wa kulia zaidi kuliko maandishi yote. ULB inafanya hivi kwa maneno yaliyotajwa kwenye mstari wa 15.

Dhana maalum katika sura hii

Zawadi kwa kanisa huko Yerusalemu

Kanisa la Korintho lilianza kutayarisha kutoa fedha kwa waumini maskini huko Yerusalemu. Makanisa ya Makedonia pia yalitoa kwa ukarimu. Paulo anatuma Tito na waumini wengine wawili huko Korintho ili kuwahimiza Wakorintho kutoa kwa ukarimu. Paulo na wengine watapeleka fedha huko Yerusalemu. Wanataka watu kujua kuwa inafanyika kwa uaminifu.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Sisi

Inawezekana kwamba Paulo anatumia neno "sisi" kuwakilisha Timotheo na yeye mwenyewe. Inaweza pia kuwajumuisha watu wengine.

Kitendawili

"Kitendawili" ni tamko la kweli ambalo linaonekana kuelezea jambo lisilowezekana. Maneno haya katika mstari wa 2 ni kitendawili: "uwingi wa furaha yao na mwisho wa umaskini wao umezalisha utajiri mkubwa wa ukarimu." Katika mstari wa 3 Paulo anaelezea jinsi umaskini wao ulivyozalisha utajiri. Paulo pia hutumia utajiri na umasikini katika vitendawili vingine. (2 Wakorintho 8:2)

<< | >>

2 Corinthians 8:1

Sentensi Unganishi

Baada ya kuwa ameeleza mipango yake iliyobadilika na mwelekeo wa huduma yake, Paulo anazungumza kuhusu utoaji.

neema ya Mungu ambayo imetolewa kwa makanisa ya Makedonia

Mstari huu waweza kuelezwa kwa jinsi ya utendaji: "neema ambayo imetolewa kwa makanisa ya Makedonia.

wingi wa furaha yao na ongezeko la umaskini wao umezaa utajiri mkubwa wa utoaji.

Paulo anazungumzia "furaha" na " umaskini: kama vile vilikuwa viumbe hai ambavyo vinaweza kutoa ukarimu.

ongezeko la umaskini wao umezaa utjiri mkubwa wa ukarimu.

Ingawa makanisa ya Makedonia yameteseka kwa majaribu ya mateso na umaskini, kwa neema ya Mungu yameweza kukusanya fedha kwa ajili waamini walioko Yerusalamu.

utajiri mkubwa wa ukarimu

" ukarimu mkubwa sana." Maneno " utajiri mkubwa" yanasisitiza ukuu wa ukarimu wao.

2 Corinthians 8:3

walitoa

Hapa ina maanisha makanisa ya Makedonia.

kwa hiari yao wenyewe

'kujitolea"

kwa kutusihi kwingi

Maneno "kutusihi" na "walituomba" hueleza maana ileile na kusisitiza uhodari amnbayo kwao watu waliwasihi.

huduma hii kwa waumini

Paulo anarejea kutoa fedha kwa waamini wa Yerusalemu.

2 Corinthians 8:6

aliyekuwa tayari ameanzisha

Paulo anaongelea fedha iliyokusanywa huko Korintho kwa ajili ya wakristo wa Yerusalemu.

kuleta katika utimilifu tendo hili la ukarimu

Tito aliwakumbusha Wakorintho kukamilisha ukusanyaji wa fedha.

Lakini ninyi mna wingi katika kila kitu

Paulo anazungumza juu ya waamini wa Korintho kama vile walikuwa wanatoa matunda ya mwuli.

hakikisheni kwamba ninyi mnakuwa na wingi pia katika tendo hili la ukarimu.

Paulo anazungumzia waamini wa Korintho kama vile wanavyopaswa kutoa matunda ya mwili "hakikisheni mnafanya vyema katika kuwahudumia waamini katika Yerusalemu."

2 Corinthians 8:8

kwa kuupima uhalisi wa upendo wenu kwa kuulinganisha na shauku ya watu wengine

Paulo anawatia moyo Wakorintho kutoa kwa ukarimu wao kwa kuulinganisha na ukarimu wa makanisa ya Makedonia.

neema ya Bwana wetu

Katika mukutadha huu neno "neema" linasisitiza ukarimu wa Yesu Kristo amewabariki Wakorintho.

Hata kama alikuwa tajiri, kwa ajili yenu alikuwa maskini

Paulo anamzungumzia Yesu kabkla hajafanyika mwanadamu alivyokuwa tajiri, na kwa kufanyika mwanadamu kama kuwa maskini.

kupitia umaskini wake mweze kuwa tajiri.

Paulo anazungumzia Wakorintho kuwa matajiri kiroho kama matokeo ya Yesu kuwa mwanadamu.

2 Corinthians 8:10

jambo hili

hii inamaanisha kukusanya mfuko kwa ajili ya wakristo wa Yerusalemu.

2 Corinthians 8:13

kwa kazi hii

Sentensi hii yaweza kuelezwa kwa jinsi hii: "alikuwa na kila kitu alichohitaji"

kwamba wengine waweze kupata nafuu na ninyi mweze kulemew

Sentensi hii yaweza kuelezwa kwa jinsi hii: : kuwa mtawaondolea wengine mzigo na kujitwisha wenyewe"

ni lazima kuwe na usawa

"lazima pawe na haki"

Hii ni hivyo pia ili kwamba wingi wao uweze kusaidia mahitaji yenu

Kwa maana Wakorintho wanatenda katika wakati uliopo, imehusishwa kuwa wakristo wa Yerusalemu kwa wakati mwingine ujao watawasaidia wao pia.

kama ilivyoandikwa

Mahali hapa Paulo ananukuu kwenye kitabu cha Kutoka.

hakupungukiwa na chochote

Sentensi hii yaweza kuelezwa hivi: "alikuwa na mahitaji yake yote"

2 Corinthians 8:16

aliyeweka ndani ya moyo wa Tito moyo uleule wa bidii ya kujali ambyo ninayo kwa ajili yenu

Neno " moyo" linamaanisha hisia. Hii ina maana kwamba Mungu alimtumia Tito kuwapenda.

moyo uleule wa bidii ya kujali

"shauku ileile au " kujihusiha kwa ndani"

Kwa kuwa si tu alipokea maombi yetu

Paulo ana maanisha ombi lake Tito kurejea Korintho na kukamilisha mchango wa fedha.

2 Corinthians 8:18

pamoja naye

"pamoja na Tito"

ndugu ambaye anasifiwa miongoni mwa makanisa

Sentensi hii yaweza kusemwa hivi: "ndugu ambaye anasifiwa miongoni mwa makanisa yote. Yaweza kusemwa hivi: "ndugu ambaye miongoni mwa waamini wa makanisa humsifu"

Si hivi tu

"Siyo waamini wote wa makanisa humsifu yeye"

lakini pia alichaguliwa na makanisa

Sentensi hii yaweza kusemwa: "yeye pia alichaguiwa na makanisa'

katika kulibeba sehemu mbalimbali tendo hili la ukarimu.

"kupeleka kwa wengine tendo hili la ukarimu " Hii ina maanisha kuchukua matoleo kupeleka Yerusalemu.

kwa shauku yetu ya kusaidia.

"kuonyesha kwa vitendo utayari kusaidia"

2 Corinthians 8:20

kuhusiana na huo ukarimu tunaoubeba

"kuhusiana na namna tunavyothibiti karama hii ya ukarimu" Hii ina maanisha kuchukua matoleo kuyapeleka Yerusalemu.

Tunachukua uangalifu kufanya kilicho cha heshima

'tunachukua uangalifu kutunza zawadi hii katika njia inayoheshimika"

mbele za Bwana, lakini pia mbele za watu.

"katika utashi wa Mungu ....katika utashi wa watu"

2 Corinthians 8:22

pamoja nao

Neno "wao"linamaanisha Tito na ndugu wengine walioorodheshwa hapa kabla.

yeye ni mshirika mwenza wangu na mtendakazi mwenzangu kwa ajili yenu

"yeye ni mshirika mwenzangu anayetenda kazi pamoja nami kwa ajili yenu"

Kama kwa ndugu zetu

Ina maanisha kwa wanume wawili wengine ambao wataungana na Tito.

wanatumwa na makanisa.

Sentensi hii yaweza kusemwa katika kauli tendaji hivi: "makanisa yamewatuma wao"

Ni waheshima kwa Kristo

Sentensi hii yaweza kusemwa katika kauli tendaji hivi: "watawasababisha watu kumheshimu Kristo"

2 Corinthians 9

2 Wakorintho 09 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri huweka kila mstari wa mashairi upande wa kulia zaidi kuliko maandiko yote ili iwe rahisi kusoma. ULB inafanya hivi kwa mstari wa 9, ambayo umechukuliwa kutoka Agano la Kale.

Mifano muhimu ya matamshi katika sura hii

Mifano

Paulo anatumia mifano mitatu ya kilimo. Anazitumia kufundisha kuhusu kutoa kwa waumini maskini. Mifano humsaidia Paulo kueleza kwamba Mungu atawapa thawabu wale wanaotoa kwa ukarimu. Paulo hakusema ni lini au vipi Mungu atakavyowapa tuzo hilo. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#reward)

<< | >>

2 Corinthians 9:1

Sentensi Unganishi

Paulo anazidi kuzungumzia juu ya somo la utoaji. Anataka kuhakikisha kuwa hayo matoleo katika sadaka zao kwa waamini wahitaji katika Yerusalemu ifanyike kabla hajaja hivyo isije ikaonekana kana kwamba anachukua fursa yao. Anazungumzia kuhusu jinsi gani utoaji unavyombariki atoaye na kumtukuza Mungu.

Habari za Jumla:

Wakati Paulo anapozungumzia Akaya, anazungumzia jimbo la Rumi lililopo kusini mwa Ugiriki mahali Korintho ilipo.

huduma kwa ajili ya waamini

Sentesnsi hii ina maanisha ukusanyaji wa fedha kuwapatia wakristo wa Yerusalamu.

Akaya imekuwa tayari

Hapa neno "Akaya" lina maanisha watu wanaoishi katika jimbo hili, Na kwa uwazi kabisa ni kwa watu wa kanisa la korintho.

2 Corinthians 9:3

hao ndugu

Paulo anazungumzia Tito na wanaume wawili wanaungana naye.

ili kwamba majivuno yetu kuhusu ninyi yasiwe ya bure

Paulo hapendi wengine wafikiri kuwa vitu ambavyo amejivunia kuhusu Wakorintho hawakuwa sahihi.

kuwakuta hamjawa tayari

"kuwakuta hamjawa tayari kuto"

sisemi chochote kuhusu ninyi

Paulo antumia sentensi kanushi kusisitiza kwamba kitu kile kile kuwa kweli kuhusu Wakorintho.

ndugu kuja kwenu

Kutoka katika mtazama wa Paulo, ndugu wanakwenda .

si kama kitu kilichoamriwa

Yaweza kuelezwa hivi: " sivyo kama kitu ambacho tuliwalazimisha kutoa"

2 Corinthians 9:6

mtu apandaye haba pia atavuna haba, na yeyote apandaye kwa lengo la baraka pia atavuna baraka

Paulo anatumia mfano wa mkulima anayepanda mbegu kufafanua matokeo ya utoaji. Kama mavuno ya mkulima inavyotegemea kiasi anachopanda, hivyo Mungu atatoa baraka kidogo au nyingi kutegemea kiasi ambacho Wakorintho wanatoa.

atoe kama alivyopanga moyoni mwake

Hapa neno "moyo" linamaanisha fikra na hisia'

si kwa huzuni au kwa kulazimishwa

Yaweza kusemwa kuwa: "kwa sababu anajisikia hatia au mtu kulmazimisha"

Kwa kuwa Mungu humpenda yule atoaye kwa furaha.

Mungu anawataka watu kutoa kwa furaha kusaidia kuwahudumia ndugu waamini.

2 Corinthians 9:8

Mungu anaweza kuwapa baraka na kuwazidishia

"Mungu ataongeza baraka kwa ajili yenu" Mtu aanayewapatia mahitaji ya kifedha waamini wengine, Mungu pia hutoa baraka zaidi kwa anayetoa. hivyo anayetoa atapokuwa na kila kitu anachohitaji.

ili kwamba muweze kuzidisha kila tendo jema.

"ili kwamba muweze kufanya matendo mema zaidi na zaidi"

kama ilivyoandikwa

"Kama iivyoandikwa" Yaweza kusemwa hivi: " "Kama vile mwandishi alivyoandika"

2 Corinthians 9:10

Naye atoaye

"Mungu atoaye"

mkate kwa ajili ya chakula

Hapa nenp "mkate" lina maanisha chakula kwa ujumla"

pia atatoa na kuzidisha mbegu yenu kwa ajili ya kupanda

paulo anazungumza mali za Wakorintho kama vile zilikuwa mbegu za kuwapa wengine kama vile wanapanda mbegu.

Yeye ataongeza mavuno ya haki yenu.

paulo analinganisha faida ambazo Wakorintho watapokea kutokana na ukarimu wao kwa mavuno hayo.

mavuno ya haki yenu

"mavuno ambayo yanatokana na matendo ya haki." Hapa neno "haki" linamaanisha matendo ya haki ya Wakorintho kwa kutoa raslimali zao kwa waamini katika Yerusalemu.

Mtatajirishwa

"Mungu atawatajirisha"

Hii italeta shukrani kwa Mungu kupitia sisi.

Neno :hii" linamaanisha ukarimu wa Wakorintho"

2 Corinthians 9:12

kwa kupeleka huduma hii

"Kwa huduma mliyofanya ya kutoa sadaka"

mahitaji ya wakristo

"mahitaji ya wakristo huko Yerusalemu"

hii pia itaongeza shukrani nyingi

"Hii itakuwa pia sababu za kila mtu kumshukuru Mungu"

kwa sababu imeonekana kwa kufanya huduma hii imekuwa kipimo kwenu

"ukarimu wenu umekuwa kipimo cha utii na upendo mlionao"

pia mtamtukuza Mungu kwa utii wenu na ukiri wa injili ya Kristo. Pi mtamtukuza Mungu kwa ukarimu wa sadaka mliotoa kwao na kwa kila mmoja.

"mtamtukuza Mungu, sio tu kwa utii wenu kwa kile mlichosema, na mnachoamini kuhusiana naye, lakini pia kwa uamuzi wa ukarimu wa kutoa sadaka kwa wakristo wote"

kwa sadaka yake isiyoelezeka

"kwa sadaka isiyoelezeka, Yesu Kristo"

2 Corinthians 10

2 Wakorintho 10 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri huweka nukuu kutoka kwenye Agano la Kale kwa upande wa kulia zaidi kuliko maandishi yote. ULB inafanya hivyo kwa maneno yaliyotajwa kwenye mstari wa 17.

Katika sura hii, Paulo anarudi kutetea mamlaka yake. Pia analinganisha jinsi anavyozungumza na jinsi anavyoandika.

Dhana maalum katika sura hii

Kujivuna

"Kujivuna" mara nyingi hufikiriwa kama kujisifu, ambayo si nzuri. Lakini katika barua hii "kujivuna" ina maana ya kujivuna kwa shukrani au kujivuna kwa furaha.

Takwimu muhimu za matamshi katika sura hii

Mifano

Katika mistari ya 3-6, Paulo anatumia mifano nyingi ya vita. Huenda anayatumia kama sehemu ya mfano kubwa juu ya Wakristo kuwa katika vita vya kiroho. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Mwili

"Labda mwili ni mfano wa asili ya dhambi. Paulo hafundishi kwamba miili yetu ni ya dhambi. Labda Paulo anafundisha kwamba wakati wote Wakristo tunapoishi ("katika mwili"), tutaendelea kutenda dhambi. Lakini asili yetu mpya itapigana dhidi ya asili yetu ya zamani. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#flesh)

<< | >>

2 Corinthians 10:1

Sentensi Unganishi

Paulo anahamisha somo kutoa katika utoaji kwenda kwenye mamlaka yake ya kufundisha kama anavyofanya.

kwa unyenyekevu na upole wa Kristo

Neno " uvimilivu" na : upole" ni majina yaliyofupishwa, na yanawea kusemwa hivi: " Mimi ni mnyenyekevu na mpole kama nifanyavyo hivyo, kwa sababu Kristo amenifanya kuwa hivyo"

Anayesadikimkuwa

"anayefikiri kuwa"

tunaishi kwa jinsi ya mwili.

Neno "mwili" ni neno linalosimama kuelezea asili ya dhambi ya mwanadamu.

2 Corinthians 10:3

tunaenenda katika mwili

Neno mwili: " ni neno mbadala lililotumika kuelezea maisha ya kimwili"

hatupigani vita ...tunapigana

Paulo anazungumzakujaribu kuwashawishi Wakorintho kumwamini na siyo waalimu wa uongo ka vile alivyokuwa akipambana vita vya mwili.

pigana vita kwa jinsi ya mwili

Maana zawezakuwa hizi: neno " mwili" ni neno linalosimama kuwakilisha maisha ya mwili" au neno "/mwili" ni neno linalosimama badala ya asili ya mwandamu ya dhambi "

silaha tunazotumia kupigana...zinaondosha kabisa mijadala inayopotosha

Paulo anazungumzia hekima ya kimungu akionyesha hekima ya kibinadamu kuwa ya uongo na kama silaha ambayo kwayo alikuwa akiharibu nguvu za adui.

si za kimwili

Maana zawezakuwa hizi: neno " mwili" ni neno linalosimama kuwakilisha maisha ya mwili" au neno "/mwili" ni neno linalosimama badala ya asili ya mwandamu ya dhambi "

2 Corinthians 10:5

kila kinachojiinua

Paulo bado anazungumza kwa fumbo juu ya neno "vita" kama vile "maarifa ya Mungu" vilikuwa jeshi na " kila kijiinuacho" ulikuwa ukuta ambao waliutengeneza kuzuia vita.

kila kitu kinachojiinua

"kila kitu ambacho huwafanya watu wajivunie"

kijiinuacho dhidi ya maarifa ya Mungu

paulo anazungumzia hoja kama vile ukuta unaosimama juu dhidi ua vita. Maneno " inuka juu" ina maanisha "simaa kwa urefu" " siyo kwamba kitu cha juu kinakuja kutoka angani.

Tunalifanya mateka kila wazo katika utii kwa Kristo

Paulo anazungumza juu ya mawazo ya watu kama vile yalikuwa askari ambaye alimteka katika vita.

kuadhibu kila matendo lisilo na uti

Maneno haya "tendo lisilo na utii" yanasimama kuwakilisha watu ambao waliyatenda maatendo hayo.

2 Corinthians 10:7

Tazameni yale yaliyo wazi mbele yenu

maana zawezakuwa: Hii ni amri au hii ni maelezo.

hebu ajikumbushe yeye mwenyewe

"yeye anahitaji kukumbuka"

"kama vile alivyo ni wa Kristo; ; hivyo ndiyo na sisi pia tuko hivyo

"kwamba sisi ni wa Krsto kama vile kwa mengi afanyayo"

kuwajenga ninyi na siyo kuwaharibu, sitaona haya

Paulo anazungumza juu ya kuwasaidia Wakorintho kujua Kristo vizuri kama vile alikuwa akijenga jengo.

2 Corinthians 10:9

mimi nawatisha

"najaribu kuwatisha ninyi"

yenye uzito na nguvu,

"iyenye uhitaji na nguvu"

2 Corinthians 10:11

Hebu watu wa jinsi hiyo wafahamu

"nawataka watu kama hao kufahamu"

kile tusemacho kwa waraka wetu wakati tukiwa mbali ni sawasawa na vile tutakavyotenda wakati tukiwa pale

"kilie tulichokikandika katika barua yetu tulipokuwa mbali nanyi"ni sawasawa na vile tutakavyotenda wakati tukiwa pamoja nanyi"

tukiwa mbali, ni sawasawa na vile tutakavyotenda wakati tukiwa pale

"tutatenda hivyo wakati tukakapokuwapo pale pamoja nanyi tulichokiandika katika barua yetu tulipokuwa mbali nanyi"

sisi..yetu

Sentensi zote za maneno haya yanarejea kwenye timu ya huduma ya Paulo na siyo Wakorintho.

kujikusanya wenyewe au kujilinganisha

"kusema tuko vizuri kama"

wanapojipima wenyewe na kujilinganisha na kila mmoja wao

Paulo anasema vitu vingi mara mbili.

wanapojipima wenyewe na kila mmoja wao

Paulo anazungumzia wema kuwa kama kilikuwa kitu ambacho urefu wake watu wangeupima.

hawana akili

"huonyesha kila mtu wasichokifahamu"

2 Corinthians 10:13

Habari za Jumla

Paulo anazungumia mamlaka aliyo nayo kama vile yalikuwa ardhi juu yake aliyoimiki, vitu vile juu yake ambachomalikuwa na mamlaka, kama kuwa kwenye mpaka au ukomo wa nchi yake , na vitu hivyo haviko chini ya mamlaka yake kama vimekuwa mbali na mipaka.

hatutajivuna kupita mipaka

Hii ni nahau au lahaja " sitajivuna juu ya vitu ambavyo sina mamlaka navyo"

ndani ya mipaka ambayo Mungu

"kuhusu vitu chini ya mamlaka ambayo Mungu"

mipaka ambayo inayofika umbali kama wenu ulivyo.

Paulo anazungumzia mamlaka aliyo nayo ka vile ardhi ambayo juu yake anaitawala.

hatukujizidishia wenyewe

"hatukuwe nda nje ya mipaka yetu"

2 Corinthians 10:15

Hatujajivuna kupita mipaka

Hii ni nahau: "hatukujivuna juu vitu ambavyo hatukuwa na mamlaka navyo"

eneo letu la kazi litapanuliwa

Sentensi hii yaweza kueleza kwa namna ya utendaji: "Mungu atazidi kupanua eneo letu la kazi"

katika maeneo mengine.

"eneo ambalo Mungu amemtuma mtu fulani"

2 Corinthians 10:17

ajivunaye ndani ya Bwana

"kijivuna juu ya kile ambacho Bwana amefanya"

ajithibitishaye mwenyewe

Hii ina maana kuwamba yule atoaye humwuliza kilamtu anayemsikia kuamua ikiwa yuko sahihi au si sahihi.

yule ambaye Bwana humthibitisha

"ambaye Bwana humthibitisha"

ni yule ambaye Bwana humthibitisha.

Unaweza kuweka wazi ufahamu wa habari: "yule ambaye Bwana himthibitisha"

2 Corinthians 11

2 Wakorintho 11 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Katika sura hii, Paulo anaendelea kutetea mamlaka yake.

Dhana maalum katika sura hii

Mafundisho ya uwongo

Wakorintho walikuwa haraka kukubali walimu wa uongo. Walifundisha mambo kuhusu Yesu na injili ambayo yalikuwa tofauti na yasiyo ya kweli. Kinyume na walimu wa uongo, Paulo aliwatumikia Wakorintho kwa moyo wake wote. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#goodnews)

Mwanga

Mwanga hutumiwa kawaida katika Agano Jipya kama mfano. Paulo hapa anatumia nuru ili kuonyesha ufunuo wa Mungu na haki yake. Giza linamaanisha dhambi. Dhambi inatafuta kubaki kufichwa kutoka kwa Mungu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#light, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#darkness and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

Mifano muhimu ya matamshi katika sura hii

Mifano

Paulo anaanza sura hii kwa mfano iliyopanuliwa. Anajilinganisha na baba wa bibi harusi ambaye anampa bintiye bikira kwa bwana harusi. Tamaduni za harusi hubadilika kulingana na historia ya kitamaduni. Lakini wazo la kumwonyesha mtu kama mtoto mzima na mtakatifu linaonyeshwa wazi katika kifungu hiki. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#holy and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

Kinaya

Sura hii imejaa kinaya. Paulo ana matumaini ya kuwaaibisha waumini wa Korintho kwa kinaya chake.

"Nyinyi huvumilia mambo haya kabisa!" Paulo anadhani kwamba hawapaswi kuvumilia jinsi mitume wa uwongo walivyowafanya. Paulo hafikiri kuwa wao ni mitume hata kidogo.

Taarifa hii, "Kwa maana mnavumilia kwa furaha wapumbavu, ninyi wenyewe ni wenye busara!" ina maana kwamba waumini wa Korintho wanadhani kama walikuwa wenye busara sana lakini Paulo hakubaliani nao.

"Nitasema kwa aibu yetu kwamba tulikuwa dhaifu sana kufanya hivyo." Paulo anazungumza kuhusu tabia anayodhani ni mbaya sana ili kuepuka. Anazungumza kana kwamba anafikiri yeye anafanya makosa kwa kutofanya hivyo. Anatumia swali la uhuishaji pia kama kinaya. "Je, nilikosa kwa kujinyenyekeza ili uweze kuinuliwa?" (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-irony and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#apostle and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-rquestion)

Maswali ya uhuishaji

Kwa kukataa mitume wa uongo wanaodai kuwa wakuu, Paulo anatumia mfululizo wa maswali ya uhuishaji. Kila swali linahusiana na jibu: "Je, wao ni Waebrania? Nami pia. Wao ni Waisraeli? Nami pia. Wao ni wazao wa Abrahamu? Nami pia. Wao ni watumishi wa Mungu? (Nazungumza kama nimepoteza ufahamu wangu.) Mimi ni zaidi."

Pia hutumia mfululizo wa maswali ya uhuishaji ili atambue shida za waumini wake wapya: "Ni nani aliye dhaifu, na mimi si dhaifu? Ni nani aliyemfanya mwingine kupotea katika dhambi, na mimi sisikiye uchungu?"

"Je, wao ni watumishi wa Kristo?"

Maneno haya ni kejeli, aina maalum ya kinaya inayotumiwa kuchokesha au kutusi. Paulo haamini kuwa walimu hawa wa uongo wanamtumikia Kristo kweli, lakini wanajifanya vile.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Kitendawili

"Kitendawili" ni tamko la kweli ambalo linaonekana kuelezea jambo lisilowezekana. Sentensi hii katika mstari wa 30 ni kitendawili: "Ikiwa ni lazima nijisifu, nitajisifu juu ya kile kinachoonyesha udhaifu wangu." Paulo haelezei kwa nini angeweza kujivunia katika udhaifu wake hadi 2 Wakorintho 12:9. (2 Wakorintho 11:30)

<< | >>

2 Corinthians 11:1

Sentensi Unganishi

Paulo anaendelea kuthibitisha utume wake.

mngevumiliana na mimi katika baadhi ya upumbavu.

"mniruhusu kutenda kama mpumbavu"

wivu...wivu

Maneno haya yanazungumzia uzuri , shauku kubwa ambayo Wakorintho wawe waaminifu kwa Kristo na kwamba hakuna mmoja anayepaswa kuwashawishi kumwacha yeye.

nilipowaahidi ninyi kwenye ndoa ya mume mmoja. Niliahidi kuwaleta ninyi kwa Kristo kama bikra safi.

Paulo anazungumzia juu ya kujali kwake kwa Waamini wa Korintho kama vile ameahidi mtu mwingine yeye angemwandaa binti yake kuolewa na yeye na zaidi ameguswa sana kwamba aweze kuitunza ahadi yake kwa mtu yule.

2 Corinthians 11:3

Lakini nina hofu kwamba kwa namna fulani....ibada safi kwa Kristo

"Lakini nina hofu kwamba kwa namna fulani wasiwasi wenu ineweza kuwatoa katika kweli na ibada safi kwa Kristo kama nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila"

mawazo yenu yanaweza kupotoshwa mbali

Paulo anazungumza kama vile walikuwa wanyama ambao watu wanaweza kuwaongoza katika njia isiyo sahihi.

kwa mfano kwamba mtu fulani akaja na

"Wakati mtu yeyote akija na"

kwa mfano kwamba mkapokea roho mwingine tofauti na yule mliyempokea. Au kwa mfano kwamba mkapokea . Au kwa mfano kwamba mkapokea injili nyingine tofauti na ile mliyoipokea

"roho tofauti na Roho Mtakatifu, au injili tofauti na ile mliyopokeamktuoka kwetu"

Mkavumilia mambo haya

"shughulikia vitu hivi"

2 Corinthians 11:5

hao wanaoitwa mitume-bora

walioitwa mitume.....Paulo anatumia maneno ya kejeli hapa kuonyesha kwamba wana umuhimu mdogo kuliko na wanavyodai kuwa"

2 Corinthians 11:7

Je, nilifanya dhambi kwa kujinyenyekeza mwenyewe ili ninyi muweze kuinuliwa

Paulo anaanza kwa kudai kwamba aliwatendea Wakorintho kwa uzuri.Swali hili la kujihoji linaweza kutafsiriwa hivi: " Nadhani tunakubaliana kwamba sikufanya dhambi kwa akujinyenyekeza mwenyewe ili ya kwamba mpate kuinuliwa"

kwa uhuru

"bila kutegemea kurudishiwa chochote kutoka kwenu"

Nilinyang'anya makanisa mengine

Sentensi hii imeelezwa kwa kuikuza au kutia chumvi kusisitiza kwamba Paulo alichukua fedha kutoka makanisa mengine.

ningeweza kuwahudumia ninyi

Maaana kamili ya sentensi hii yaweza kuwa: "Naweza kuwatumikia ninyi bila gharama"

Katika kila kitu nimejizuia mwenyewe kutokuwa mzigo kwenu

"sijawahi kwa njia yoyote kuwa mzigo kwenu kifedha.

ndugu waliokuja

"Ndugu hawa" huenda walikuwa wanaume wote.

2 Corinthians 11:10

Kama kweli ya Kristo ilivyo ndani yangu, huki

Paulo anasisitiza hiki kwa sababu wasomaji wake wanajua kuwa anawaambia kweli ya Kristo, wanaweza kujua kuwa mahali hapa anawaambia ukweli.

huku kujisifu kwangu hakutanyamazishwa

Sentensi hii yaweza kusemwa hivi: "hakuna hata mmoja atakayeweza kunizuia kujisifu na kukaa kimya. "Paulo "anajivuna" kuwa yuko "huru kuhubiri injili"

sehemu za Akaya

"mikoa ya Akaya" Neno "sehemu" linazungumzia maeneo ya nchi , na siyo mgawanyo wa kisiasa.

Kwa nini? Kwa sababu siwapendi?

Paulo anatumia swalimla kujihoji kusisitiza upendo kwa Wakorintho.

Mungu anafahamu

Kwa kuweka wazi sentensi hii: "Mungu anajua Ninawapenda"

2 Corinthians 11:12

Sentensi Unganishi

Kwa kuwa Paulo anaendelea kuthibitisha kwamba utume wake, anazungumzia kuhusu mitume wa uongo.

ili kwamba niweze kuondoa madai

Paulo anazungumzia madai ya manabii wa uongo kuwa hali ya maadui wake kama ilikuwa kitu anachoweza kukiondoa"

wanataka kujivuna kwa lipi?

Wakati kujisifu kwa Paulo kulikuwa "uhuru kuhubiri injili"

wameonekana wakifanya kazi ile ile ambayo tunaitenda

Hii ina maana kwamba "wale watu watafikiri kuwa wako kama sisi"

kwa watu wa jinsi ile

"Ninafanya yale ninayoyafanya kwa sababu watu wanayapenda"

watendakazi wadanganyifu

"wafanya kazi wasio heshimiwa"

Wanajifanya wenyewe kama mitume

""siyo mitume, lakini wanajaribu wao wenyewe kuwa kama mitume"

2 Corinthians 11:14

Na hii haishangazi...Hii haina mshangao mkubwa kama

kwa kusema hivi, huu ni mtazamo hasi Paulo anasisitiza kuwa Wakorintho wanpaswa kutarajia kukutana na "mitume wengi wa uongo"

Shetani hujigeuza mwenyewe kama malaika wa nuru

"Shetani siyo malaika wa nuru, akini hujaribu kujifanya mwenyewe kuwa kama malaika wa nuru"

watumishi wake pia kujigeuza wenyewe kama watumishi wa haki.

"watumishi wake siyo watumishi wa haki, lakini hujaribu kujifanya wenyewe kuwa kama watumishi wa haki"

2 Corinthians 11:16

nipokeeni mimi kama mpumbavu ili niweze kujisifu kidog

"nipokee mii kama vile ungempokea mpumbavu:niache mimi nizungumze, na kufikiri kujivuna kwangu maneno ya mpumbavu"

Kile ninachosema kuhusu huku kujiamini kwa kujivuna hakuhukumiwi na Bwana

Sentensi hii yaweza kuelezwa kwa jinsi hii: " "Bwana hajifanyi kutoona ninacho kiongelea kuhusu ujasiri wa kujivuna" Bwana hajaniambia kuwa ana thibitisha kwa kile ninachokizungumza huu ujasiri wa kujisifu.

kwa jinsi ya mwili

Katika sentensi hii mbadala wa neno "mwili" una maanisha mtu katika asili yake yha dhambi na maendeleo yake.

2 Corinthians 11:19

mlichukuliana na wapumbavu

"nikubali mimi ninapotenda kama mpembavu"

ninyi wenyewe mna busara

Paulo ana waaibisha Wakorintho kwa ktumia kinyume au kejeli.

akikutia utumwani

Paulo anazungumzia juu ya sheria ambazo Mungu hakuzifanya lakini baadhi ya watuwaliwalazimisha wengine kutii kana kwamba ilikuwa utumwa.

yeye huwaharibu ninyi

Paulo anazungumzia juu ya utume ulio bora kuchukua raslimali ya vitu vya watu kana kwamba ilikuwa kuwala watu wenyewe.

akiwatumia ninyi kwa faida yake

Mtu anayechukua fursa ya mtu mwingine kwa kujua vitu ambavyo mtu mwingine havifahamu, na kuyatumia hayo maarifa kumsaidia yeye mwenyewe na kumwumiza mtu mwingine.

Nitasema kwa aibu yetu kwamba sisi tukuwa dhaifu sana kufanya hivyo

Kwa aibu ninakiri kwamba hatukuwa wenye nguvu vya kutosha kuwatendae ninyi hivyo. Paulo anatumia neno la kinyume kuonyesha kuwa siyo kwa sababu alikuwa dhaifu hivyo aliwatendea wao vizuri.

Na bado kama yeyote akijivuna.... mimi pia nitajivuna.

"vyovyote mtu akijisifu, juu ya....mimi pia sitaogopa kufanya hivyo"

2 Corinthians 11:22

Sentensi Unganishi

Vile Paulo anaendelea kuthibitisha utume wake, anazungumza vitu vya wazi ambavyo vimetokea kwake tangu alipo kuwa mwamini.

Je, wao ni Waisraeli?..Je, wao ni Waisraeli?..Je, wao ni uzao wa Abrahamu?...Je, wao ni watumishi wa Kristo?...(Nanena kama nilikuwa nimechanganyikiwa.) Mimi ni zaidi

Paulo anauliza maswal Wakorintho wanaweza kuwa walikuwa wanauliza na tena kuwajibu kusisitiza kuwa yeye ni myahudi zaidi -kama walivyo mitume bora.

kana kwamba kama nilikuwa nimechanganyikiwa

"kana kwamba nilikuwa siwezi kufikiri vizuri"

Mimi zaidi

Inaweza kuwekwa wazimkwa kusema "Mimi ni mtumishi wa Kristo zaidi kuliko walivyo"

hata katika kazi ngumu

"nimefanya kazi ngumu"

mbali zaidi ya kuwa vifungoni,

"nimekuwa vifungoni mara nyingi"

katika kupigwa kwingi

Hiki ni nahau na imetumika kuelezea kwa undani msisitizo mara ngapi yeye amepigwa,

katika kukabili hatari nyingi za kifo.

"na karibia nife mara nyingi"

2 Corinthians 11:24

mapigo arobaini kasoro moja

hii ilikuwa kawaida kueleza kuwa nimechapwa viboko 39. Viboko arobaini[40] inadhaniwa ni kuua mtu.

Nilipigwa kwa fimbo

Sentensi hii yaweza kuelezwa kwa kauli tendaji hivi: "watu walinipiga kwa viboko vya miti"

"nilipigwa kwa mawe"

Sentensi hii yaweza kuelezwa kwa jinsi hii:"watu walinitupia mawe mpaka wakadhania kuwa nimekufa"

Nimetumia usiku na mchana katika bahari wazi

Paulo anazungumzia muda aliokuwa majini wakati meli ilipokuwa katika kuzama.

hatarini kwa ndugu za uongo

"na hatari toka kwa wanaojifanya kuwa ndugu katika Kristo, lakini ni wametusaliti"

2 Corinthians 11:27

na uchi

Katika sentensi ina maanisha "na kukosa nguo ya kunitia joto"

nani ni dhaifu, na mimi siyo dhaifu?

Hili ni swali la kujihoji linaloweza kutafiriwa kam ifuatavyo: Wakati mtu yeyote akiwa dhaifu, na mimi najisikia nina udhaifu pia."

kuna msukumo wa kila siku juu yangu wa wasiwasi wangu

Paulo anafahamu kwamba Mungu atamshikilia kuwajibika kwa jinsi makanisa yanavyomtii Mungu na anazungumza juu ya yale maarifa kama vile yalikuwa mzigo mzito wa kitu kinacho msukuma chini.

Nani ni dhaifu, na mimi siyo dhaifu?

Neno "dhaifu"huenda ni mfano kelezea hali ya kiroho. Lakini hakuna hata mmoja anajua kwa hakika paulo anazungumzia nini!

Nani amesababisha mwingine kuanguka

Paulo anatumia swali hili kuonyesha hasira yake wakati mmwamini amesababishwa kutenda dhaambi.

amesababisha kuanguka

Paulo anazungumzia juu ya dhambi ilikuwa kitu kitu fulani kinatchotembea na hatimaye kuanguka.

mimi siungui

Paulo anazungumzia kwa hasira juu ya dhambi kama vile alikuwa na moto ndani ya mwili wake.

2 Corinthians 11:30

kwamba inachoonyesha udhaifu wangu

"jinsi nilivyo na udhaifu" "kinachoonyesha jinsi nilivyo dhaifu"

mimi sidanganyi

Paulo anatumia sentensi yenye nguvu na ya ukanusho kusisitiza maana katika mtazamo wa kukubali.

2 Corinthians 11:32

Kule Dameski, mkuu wa mkoa chini ya mfalme Areta alikuwa akiulinda mji

"mkuu wa mkoa ambaye aliteuliwa na mfalme Areta aliwaambia wanaume kuulinda mji"

kwa kunikamata mimi

"hivyo wanaweza kunivizia na kunikamata"

niliwekwa kwenye kikapu

Sentensi hii yaweza kuelezwa hivi: "watu baadhi waliniweka ndani ya kikapu na kunishusha chini"

kutoka mikononi mwake

Paulo anatumia mikono ya mkuu wa mkoa kama mfano kwa mkuu wa mkoa .

2 Corinthians 12

2 Wakorintho 12 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Paulo anaendelea kutetea mamlaka yake katika sura hii.

Wakati Paulo alikuwa pamoja na Wakorintho, alijitokeza kuwa mtume kwa matendo yake yenye nguvu. Yeye hakuwahi kuchukua chochote kutoka kwao. Sasa kwa vile anakuja kwa mara ya tatu, bado hatachukua chochote. Anatarajia kwamba atakapowatembelea, hatahitaji kuwa mkali kwao. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#apostle)

Dhana maalum katika sura hii

Maono ya Paulo

Paulo sasa anatetea mamlaka yake kwa kusema juu ya maono mazuri ya mbinguni. Ingawa anazungumza kama mtu wa tatu katika mistari ya 2-5, mstari wa 7 unaonyesha kwamba alikuwa mtu aliyepata maono. Ilikuwa kubwa sana kiasi cha Mungu kumpa ulemavu ili kumfanya awe mnyenyekevu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#heaven)

Mbingu ya tatu

Wasomi wengi wanaamini kuwa mbingu "ya tatu" ndiyo makao ya Mungu. Hii ni kwa sababu Maandiko pia hutumia "mbingu kutaja anga (mbingu ya kwanza) na ulimwengu kutaja mbingu ya pili").

Mifano muhimu ya matamshi katika sura hii

Maswali ya hekima

Paulo anatumia maswali mengi ya uhuishaji anapojitetea dhidi ya maadui zake ambao walimshtaki: "Kwa nini mlikuwa wa hadhi ya chini zaidi kuliko makanisa yote, isipokuwa kwamba sikuwa mzigo kwenu?" "Je, Tito aliwatoza kitu? Je, hatukutembea kwa njia ile ile? Je, hatukuenda kwa hatua moja?" na "Je, unadhani wakati huu wote tumejitetea kwako?" (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-rquestion)

Kejeli

Paulo anatumia kejeli, aina ya kinaya, wakati anapowakumbusha jinsi alivyowasaidia bila gharama. Anasema, "Nisamehe kwa makosa haya!" Pia hutumia kinaya ya kawaida wakati anasema: "Lakini, kwa kuwa mimi ni mwangalifu, mimi ndiye niliyekukuta kwa udanganyifu." Anaitumia kuanzisha utetezi wake dhidi ya mashtaka haya kwa kuonyesha jinsi ambavyo haingewezekana kuwa kweli. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-irony)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Kitendawili

"Kitendawili" ni tamko la kweli ambalo linaonekana kuelezea jambo lisilowezekana. Sentensi hii katika mstari wa 5 ni kitendawili "Sitajisifu, ila juu ya udhaifu wangu." Watu wengi hawajisifu kuhusu kuwa dhaifu. Sentensi hii katika mstari wa 10 pia ni kitendawili: "Maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu." Katika mstari wa 9, Paulo anaeleza kwa nini maneno haya yote ni ya kweli. (2 Wakorintho 12: 5)

<< | >>

2 Corinthians 12:1

Sentensi Unganishi

Paulo anatetea utume wake kutoka kwa Mungu, paulo anaendelea kusema wazi mambo yale yaliyompata tangu awe mwamini.

Nitaendelea

"nitaendelea kuzungumza, hata sasa juu yake"

maono na mafunuo kutoka kwa Bwana

Maana zaweza kuwa hizi" Paulo anatumia maneno "maono" na "mafunuo" kumaanisha kitu kile kile kimeunganishwa kwa maneno tofauti ili kutoa msisitizo.

Namjua mtu mmoja katika Kristo

Paulo kwa hakika anajisema yeye mwenyewe kama vile alikuwa mtu mwingine, lakini hii ikiwezekana ni lazima itafsiriwe kama ilivyoandikwa.

ikiwa katika mwili, au nje ya mwili, mimi sijui

Paulo anazidi kujieleza yeye mwenyewe kama ikiwa hii itatokea kwa mtummwingine.

Mungu anajua

"ni Mungu pekee ajuaye"

mbingu ya tatu

Hii inalelezea mahali anapokaa Mungu na siyo mbingu au nafasi wazi angani (sayari, nyota, na dunia)

2 Corinthians 12:3

Habari za Jumla:

Paulo anazidi kujizungumzia yeye mwenyewe ingawa kama vile alikuwa anazungumzia mtu mwingine

mtu huyu alichukuliwa juu hadi paradiso

Sentensi hii yaweza kuelezwa kwa jini hii: Maana zinazowezekana: "Mungu tazama mtu huyu...katka paradiso" au "malaika alimchukua mtu huyu .

alichukuliwa juu

ghafla na kwa kulazimishwa alifanyika na kuchukuliwa

Paradiso

Maana zinazoezekana ni hizi" mbibuni au mbingu ya tatu au sehemu maalumu mbinguni.

kwa niaba ya mtu kama huyo

"kwa niaba ya mtu huyo"

sitajisifu, isipokuwa kuhusu udhaifu wangu

Sentensi hii yaweza kusemwa hivi: "Nitajivuna tu kwa udhaifu wangu"

2 Corinthians 12:6

Sentensi Unganishi

Kama vile Paulo anavyotetea utume wake kutoka kwa Mungu, anawaambia juu ya udhaifu ambao Mungu alimpa yeye kumfanya awe mnyenyekevu.

Habari za Jumla:

Wakati paulo anazungumza juu ya "mwiba katika mwili wake"; anaonyesha kuwa yeye ni "mwanadamu"

kusikika kutoka kwangu. Sitajivuna pia kwa sababu ya hayo mafunuo ya aina ya ajabu. Kwa hiyo, hivyo sitajawa na kiburi, mwiba

Maana nyingine ni hii;' " kusikia kutoka kwangu. Kwa hiyo, hivyo sitajawa na kiburi kwa sababu ya aina ya mafunuo hayo, mwiba."

kwa sababu ya hayo mafunuo ya aina ya ajabu. Kwa hiyo, hivyo sitajawa na kiburi, mwiba

Maana nyingine ni hii;' " kusikia kutoka kwangu. Kwa hiyo, hivyo sitajawa na kiburi kwa sababu ya aina ya mafunuo hayo, mwiba."

Kwa hiyo, hivyo sitajawa na kiburi,

"kunifanya mimimnisijawe na kiburi"

kijawa na

kujazwa na hewa na kuwa kubwa mno kuliko ilivyo kawaida

mwiba katika mwili

Haapa matatizo ya Paulo ya mwili yamelinganishwa na "mwiba" unaochoma "mwili wake"

mjumbe wa shetani

"mtumishi wa shetani"

kunishambulia mimi

"kunitesa mimi"

2 Corinthians 12:8

mara tatu

Paulo anayaweka maneo haya mwanzo wa sentensi kusisitiza kuwa ameomba mara nyingi kuhusu "mwiba wake"

Bwana kuhusu kuhusu hili

"Bwana kuhusu mwiba huu ndani ya mwili" au "Bwana kuhusu teso hili"

Neema Yangu yakutosha

"nitakuwa mnyenyevu kwako, na hivyo ndivyo unavyohitaji"

kwa kuwa nguvu hufanywa kamili katika udhaifu.

"kwa kuwa nguvu zangu zinafanya kazi vizuri wakati ukiwa dhaifu"

uweza wa Kristo uweze kukaa juu yangu

Paulo anazungumza juu ya "nguvu za Kristo" kuwa ilikuwa kama hnema lililojengwa juu yake."Watu wanaweza kuona kuwa ninazo nguvu za Kristo" au "Nitaweza kwa hakika kuwa na uweza wa Kristo."

ninatosheka kwa ajili ya Kristo, katika udhaifu, katika matukano, katika shida, katika mateso, katika hali ya masikitiko

Maana zawezakuwa"Nina utoshelevu katika udhaifu, katika matukano, katika shida, katika mateso, katika hali ya masikitiko kama vitu hivi vinakuja kwa sababu mimi ni wa Kristo" au "Nina utoshelevu katika udhaifu....kama vitu hivi vinawafanya watu kumjua Kristo"

katika udhaifu

"wakati ninapokuwa katika udhaifu"

katika matukano

"wakati watu wanapojaribu kunifanya nikasirike kwa kusema kwamba mimini mtu mbaya"

katika shida

"wakati ninapoteseka"

katika hali ya masikitiko

"wakati kuna mateso"

wakati nikiwa dhaifu, kisha nina nguvu

Paulo anasema hivyo wakati anapokuwa hana nguvu za kutosha kufanya yale ambayo anahitajika kuyafanya, Kristo aliye na nguvu zaidi kuliko Paulo angeweza kuwa, atafanya kazi kwa njia ya Paulokufaya yale anayohitaji kufanya.Hata hivyo, itakuwa vyema zaidi kuyatafsiri maneno haya kama yalivyoandikwa, kama lugha yako inaruhusu.

2 Corinthians 12:11

Sentensi Unganishi

Paulo anawakumbusha waamini wa Korintho juu ya ishara za kweli za mtume na uvumilivu wake mbele zao kuwatia nguvu.

Mimi nimekuwa mpumbavu

"ninatenda kama mpumbavu"

mlinilazimisha kwa hili

"mlinilazimisha kuongea kwa njia hii"

nilipaswa kusimesifiwa na ninyi.

"ni sifa ambayo mlipaswa kunipa"

sifa

" Ina maanisha "sifa" na "kushuhudiwa"

Kwa kuwa sikuwa duni

"kwa kutumia kauli ya kukanusha, anasema kwa nguvu kwamba hao wakorintho wanaodhani kuwa yuko duni hawako sahihi.

mitume--bora

Mitume-Paulo anatumia neno hili kwa kejeli kuonyesha kuwa hawana umuhimu kama wanavyodai.

Ishara za kweli za mtume zilifanyika

Sentensi hii ionaweza kutafsiriwa katika kauli tendaji pamoja na msisitizo juu ya "ishara"

ishara....ishara

Tumia maneno yote kwa wakati mmoja

ishara na maajabu

Kuna ishara za "kweli za mitume" ambazo Paulo alizitenda kwa uvumilivu mwingi.

Kwa namna gani mlikuwa wa muhimu wa chini kuliko makanisa... isipokuwa ...ninyi

Paulo anasisitiza kuwa Wakorintho wanafanya makosa kumshitaki Paulo kwa kutaka kuwaumiza.

sikuwa mzigo kwenu

"sikuwaomba pesa au vitu vingine nilivyohitaji"

Mnisamehe kwa kosa hili

Paulo amekuwa mwenye kukejeli kuwaaibisha Wakorintho. Pia yeye na wao wanajua kuwa hajafanya baya lolote, lakini wanamfikiria kuwa kama amewakosea

kwa kosa hili

kuto waomba pesa na mahitaji mengine aliyohitaji

2 Corinthians 12:14

Nawataka ninyi

"Ninachihitaji ni kwamba mnipende na kunikubali"

watoto hawapaswi kuweka akiba kwa ajili ya wazazi.

Watoto wadogo hawawajibiki kutunza fedha kwa afya za wazazi wao.

Nitafurahi zaidi kutumia

Pailo anazungumzia kazi yake na maisha yake ya mwili kama vile ilikuwa fedha ambazo yeye au Mungu angetumia.

kwa ajili ya nafsi zenu

Neno 'roho" ni linawakilisha watu wenyeywe.

Kama ninawapenda zaidi, natakiwa kupendwa kidogo?

Swali hili lakujihoji linaweza kutafsiriwa hivi: "Kama niawapenda ninyi sana, ninyi hampaswi kunipenda mimi kidogo.

zaidi

Haiko bayana nini Paulo kusema " pendo la Paulo ni zaidi"

2 Corinthians 12:16

Lakini, kwa kuwa mimi ni mwerevu, nimekuwa ambaye niliwapata kwa udanganyifu

Paulo anatumia neno la kejeli kuwaaibisha Wakorintho wanaofikiri naliwadanganya hata kama hakuwaomba pesa.

Nilichukua kitu kwenu kupitia kwa mtu yeyote niliyemtuma?

"Hakuna mtu niliyemtuma akachukua kitu kwenu!"

Je Tito alichukua kitu kwenu?

"Tito hakuchukua kitu kwenu."

Hatukuenenda kwa mwenendo ule ule?

"Sote tulikuwa na tabia na maisha yanayofanana."

Hatukuenenda kwa namna ileile?

"Sote tulifanya kwa namna inayofanana."

2 Corinthians 12:19

Sasa mnafikiri kwa hayo yote tunajitetea kwenu?

Paulo alifafanua kwamba hajitetei kwao kwa tabia yake. "Msifikiri kwamba kwa hayo wakati huu najitetea mwenyewe kwenu."

Mbele za Mungu,

Paulo anazungumzia juu ya ufahamu wa Mungu kufahamu mambo yote Paulo anafahamu pia kama vile Mungu alikuwa pa kimwili na amechunguza kila kitu alichosema na kufanya Paulo.

kwa ajili ya kuwaimarisha ninyi

"ya kwamba muweza kumjua Mungu na kumtii yeye vizuri"

2 Corinthians 12:20

Naweza nisiwakute kama ninavyotaka

"Sitapenda vile nitakavyowakuta"

ninyi mnaweza msinikute kama mnavyotaka

"mnaweza msipende majibu yangu"

Nina hofu kwamba mnaweza msinipate mimi kama mnavyotamani. Nahofia kwamba kunaweza kuwa na majadiliano, wivu, milipuko ya hasira, tamaa ya ubinafsi, umbeya, kiburi, na ugomvi

"baadhi yenu mnaweza kuwa mnagombana na sisi, wenye wivu na sisi, ghafla wenye chuki na sisi, mnazungumza kuhusu mambo yetu ya binafsi, wenye kiburi, na kutupinga sisi tunapojaribu kuwaongoza". "baadi yenuwatakuwa wenye kugombana na kila mmoja, wenye wivu na kila mmoja, ghafla mnakuwa wenye hasira na kila mmoja wenye kiburi, na kuwapinga ambao Mungu amewachagua kuongoza"

Nitahuzunika kwa hao waliotenda dhambi tangu sasa

Nitakuwa na huzuni kwa sababu wengi wao hawakutubu dhambi zao za zamani"

hawakutubu kwa uchafu na uasherati na ufisadi na anasa waliokwisha zoea

"na hawakutubu kwa dhambi ile ya uasherati waliyoizoea" au "Paulo anazungumzia juu ya aina tatu za dhambi."

mambo ya uchafu

"ya mambo ya kufikiri kwa siri juu yake na kutamani vitu ambavyo havimpenfezi Mungu"

mambo ya uasherati

"kufanya mambo ya uzinzi"

mambo ya tamaa

"ya kufikiri mkwa siri juu yake na na kutamani vitu ambavyo havimpendzi Mungu"

2 Corinthians 13

2 Wakorintho 13 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Katika sura hii, Paulo anamaliza kutetea mamlaka yake. Kisha anahitimisha barua hii kwa salamu ya mwisho na baraka.

Dhana maalum katika sura hii

Maandalizi

Paulo anawaeleza Wakorintho anapojitayarisha kuwatembelea. Anatumaini kuepuka tatizo ya kumwadhibu yeyote kanisani ili aweze kuwatembelea kwa furaha. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#disciple)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Nguvu na udhaifu

Paulo kila mara anatumia maneno tofauti "nguvu" na "udhaifu" katika sura hii. Mtafsiri anapaswa kutumia maneno mawili ya tofauti kabisa.

"Jichunguzeni na muone kama mko katika imani. Mjijaribu wenyewe."

Wasomi wamegawanyika juu ya maana ya maneno haya. Wasomi wengine wanasema kwamba Wakristo wanapaswa kujijaribu wenyewe ili kuona kama matendo yao yanahusiana na imani yao ya Kikristo. Wasomi wamegawanyika juu ya maana ya maneno haya. Wasomi wengine wanasema kwamba Wakristo wanapaswa kujijaribu wenyewe ili kuona kama matendo yao yanahusiana na imani yao ya Kikristo. Muktadha unapendeza ufahamu huu. Wengine wanasema maneno haya yanamaanisha kuwa Wakristo wanapaswa kuangalia matendo yao na kuuliza kama wameokolewa kwa kweli. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#save). Wengine wanasema maneno haya yanamaanisha kuwa Wakristo wanapaswa kuangalia matendo yao na kuuliza kama wameokolewa kwa kweli. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#save)

__<< | __

2 Corinthians 13:1

Sentensi Unganishi

Paulo anathibitisha kuwa Kristo anazungumza kupitia yeye na kwamba Paulo anangojea kuwahuisha, kuwatiamoyo, na kuwaunganisha wao.

Kila shitaka

Amini kwamba mtu fulani amefanya vibaya ni watu wawili au watatu tu wameshuhudia jambo lile lile.

wote waliosalia

'ninyi watu wote wengine "

2 Corinthians 13:3

alisulibiwa

walimsulibisha

lakini tutaishi naye kwa nguvu za Mungu

Mungu hupa nguvu na uwezo wa kuishi maisha ndani yake pamoja naye.

2 Corinthians 13:5

Jipimeni wenyewe...hamjagundua...haijagundulika

Maneno "gundulika" na "haijagundulika" yanaweza kuwa na maana ya kupitisha au kutopitisha jaribu.

ninyi hamkubali kwamba Yesu Kristo yu ndani yenu?

"ninyi mnapaswa kujua kuwa Yesu Kristo yumo ndani yenu"

ndani yenu

Inawezekana inamaanisha 1) anaishi ndani ya mtu binafsi au 2) "katikati yenu, "na sehemu muhimu zaidi ni wafuasi wa kundi.

sisi hatukukataliwa

"Hakika sisi tumekubaliwa."

2 Corinthians 13:7

kwamba msifanye neno lolote baya

"msitende dhambi kwa jambo lolote" "kwamba muweze kutenda mambo yote kwa haki."

muweze kushinda majaribu

"tuwe walimu na tuishi katika kweli"

hatuwezi kufanya jambo lolote kinyume na kweli

"hatuwezi kuwazuia watu katika kujifunza ukweli'

ukweli...lakini ni kwa ajili ya kweli tu.

"kila kitu tukifanyacho kitawasaidia watu kujifunza ukweli"

2 Corinthians 13:9

muweze kuwa timilifu

"muweze kukomaa kiroho"

katika kutumia mamlaka yangu

"wakati ninapotumia mamlaka yangu"

ya kwamba nipate kuwawajenge na siyo kuwaharibu chini

Paulo anazungu,zia juu ya kuwasaidia Wakorintho kumjua Kristo vizuri kama vile alikuwa akijenga jengo.

2 Corinthians 13:11

Sentensi Unganishi

Paulo anafunga barua hii kwa waamini Wakorintho.

fanyeni kazi kwa ajili ya urejesho

"tenda kazi kufikia ukomavu"

kubalianeni ninyi kwa ninyi

"muishi kwa mahusiano mazuri na kila mtu"

kwa busu takatifu

"kwa upendo wa Kikristo"

Utangulizi wa Wagalatia

Sehemu ya 1: Utangulizi wa Ujumla

Maelezo ya Kitabu cha Wagalatia

  1. Paulo anatangaza mamlaka yake kama mtume wa Yesu Kristo; anasema kwamba anashangazwa na mafundisho ya uongo ambayo Wakristo wa Galatia wamekubali kutoka kwa watu wengine (1:1-10).
  2. Paulo anasema kwamba watu wanaokolewa kwa kumtegemea Kristo pekee, si kwa kushika sheria (1:11-2: 21).
  3. Mungu anaweka watu kuwa haki na yeye wakati wanapomwamini Kristo tu; mfano wa Abrahamu; laana ambayo sheria huleta (na sio njia ya wokovu); utumwa na uhuru uliolinganishwa na kuonyeshwa nao Hagari na Sara (3:1-4:31).
  4. Watu wanapojiunga na Kristo, huwa huru kutokana na kuzingatia sheria ya Musa. Wao pia wako huru kuishi kama Roho Mtakatifu anavyowaongoza. Wao wako huru kukataa madai ya dhambi. Wao wako huru kubeba mizigo ya wenzao (5:1-6:10).
  5. Paulo anawaonya Wakristo wasiamini katika kutahiriwa na kufuata sheria ya Musa. Lakini, wanapaswa kumtegemea Kristo (6:11-18).

Nani aliandika Kitabu cha Wagalatia?

Paulo aliandika 1 Wakorintho. Paulo alitoka mji wa Tarso. Alikuwa alijulikana kwa jina la Sauli katika maisha yake ya awali. Kabla ya kuwa Mkristo, Paulo alikuwa Mfarisayo. Aliwatesa Wakristo. Baada ya kuwa Mkristo, alisafiri mara kadhaa katika Ufalme wa Roma akiwaambia watu kuhusu Yesu.

Haijulikani wakati gani Paulo aliandika barua hii na mahali gani alikuwa wakati wa kuandika. Wasomi wengine wanafikiri Paulo alikuwa katika mji wa Efeso na aliandika barua hii baada ya safari yake ya pili kuenda kuwaambia watu kuhusu Yesu. Wasomi wengine wanafikiri Paulo alikuwa katika mji wa Antiokia huko Siria na akaandika barua baada ya safari yake ya kwanza.

Kitabu cha Wagalatia kinahusu nini?

Paulo aliandika barua hii kwa Wakristo Wayahudi na Wayunani katika eneo la Galatia. Alitaka kuandika dhidi ya walimu wa uongo ambao walisema kwamba Wakristo wanahitaji kufuata sheria ya Musa. Paulo alitetea injili kwa kueleza kwamba mtu anaokolewa kwa kuamini Yesu Kristo. Watu wanaokolewa kama matokeo ya Mungu kuwa wema na sio matokeo ya watu wanaofanya kazi nzuri. Hakuna mtu anayeweza kumtii kikamilifu sheria. Jaribio lolote la kumpendeza Mungu kwa kuitii sheria ya Musa litasababisha Mungu kuwahukumu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#goodnews, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#save, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lawofmoses and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#works)

Je, kichwa cha kitabu hiki kinapaswa kutafsiriwaje?

Watafsiri wanaweza kuchagua kuita kitabu hiki kwa kichwa chake cha jadi, "Wagalatia." Au wanaweza kuchagua kichwa cha wazi zaidi, kama "Barua ya Paulo kwa Kanisa la Galatia." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-names)

Sehemu ya 2: Dhana muhimu za Kidini na za Kitamaduni

Ina maana gani "kuishi kama Wayahudi" (2:14)?

"Kuishi kama Wayahudi" inamaanisha kutii sheria ya Musa, ingawa mtu anategemea Kristo. Watu kati ya Wakristo wa kwanza ambao walifundisha kwamba hii ilikuwa muhimu waliitwa "Wayudaiza".

Sehemu ya 3: Masuala muhimu ya Tafsiri

Paulo alitumiaje maneno "sheria" na "neema" katika Kitabu cha Wagalatia?

Maneno haya hutumiwa kwa njia ya pekee katika Wagalatia. Kuna fundisho muhimu katika Wagalatia kuhusu maisha ya Kikristo. Chini ya sheria ya Musa, maisha ya haki au matakatifu yalihitaji mtu kuitii kanuni na masharti. Kama Wakristo, maisha matakatifu sasa yamehamasishwa na neema. Hii inamaanisha kwamba Wakristo wana uhuru katika Kristo na hawatakiwi kutii masharti ya binadamu. Lakini Wakristo wanapaswa kuishi maisha matakatifu kwa sababu wanashukuru kwamba Mungu amekuwa mwenye huruma kwao. Hii inaitwa "sheria ya Kristo." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#holy)

Paulo alimaanisha nini kwa maneno "katika Kristo," "katika Bwana," nk?

Aina hii ya kujieleza ipo katika 1:22; 2:4, 17; 3:14, 26, 28; 5:6, 10. Paulo alijaribu kueleza wazo la muungano wa karibu sana sana kati ya Kristo na waumini. Lakini, aldhamiria maana maana nyingine pia. Angalia, kwa mfano, "tunapomtafuta Mungu kutuhakikisha katika Kristo" (2:17), ambako Paulo alizungumzia kuwa mwenye haki kwa njia ya Kristo.

Tafadhali angalia utangulizi wa Kitabu cha Warumi kwa maelezo zaidi juu ya aina hii ya kujieleza.

Je, ni masuala gani muhimu katika Kitabu cha Wagalatia?

Kifungu kinachofuata ni suala la maana zaidi katika Kitabu cha Wagalatia:

Galatians 1

Wagalatia 01 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Paulo alianza barua hii tofauti na barua zake zingine. Anaongezea kwamba yeye "hakuwa mtume kutoka kwa wanadamu wala kwa shirika la kibinadamu, bali kupitia Yesu Kristo na Mungu Baba, aliyemfufua kutoka kwa wafu." Paulo labda alijumuisha maneno haya kwa sababu walimu wa uongo walimpinga na kujaribu kushusha mamlaka yake.

(note title)

Dhana maalum katika sura hii

Uzushi

Mungu milele huwaokoa watu kupitia injili ya kweli, ya kibiblia, tu. Mungu anakataa namuna lolote lingine la injili. Paulo anamwomba Mungu kuwalaani wale wanaofundisha injili ya uwongo. Huenda wasiokolewe. Wanapaswa kutendewa kama wasio Wakristo. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#save, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#eternity, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#goodnews and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#condemn and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#curse)

Tabia za Paulo

Watu wamoja katika kanisa la kwanza walikuwa wakifundisha kwamba Wayunani walistahili kutii sheria ya Musa. Ili kukataa mafundisho haya, katika mistari ya 13-16 Paulo anaeleza jinsi zamani alikuwa Myahudi mwenye bidii. Lakini Mungu bado alikuwa anahitaji ya kumwokoa na kumwonyesha injili ya kweli. Kama Myahudi, na mtume kwa Wayunani, Paulo alikuwa na tabia ya sifa ya pekee ya kukabiliana na suala hili. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lawofmoses)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Mnaacha upesi hivi na mnafuata injili ya namuna nyingine"

Kitabu cha Wagalatia ni mojawapo ya barua za kwanza za Paulo katika Maandiko. Inaonyesha kwamba vita vya uzushi vilikuwepo hata katika kanisa la kwanza. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

| >>

Galatians 1:1

Sentensi unganishi

Mtume Paulo, mwandishi wa barua hii kwa makanisa yaliyoko katika maeneo ya Galatia.

Maelezo ya jumla

Maneno 'ninyi,' 'nanyi' au 'yenu' hurejelea watu wa Galatia katika wingi wao.

Aliyemfufua yeye

"Aliyemfufua Yesu Kristo"

Kufufuliwa

Hapa inamaanisha ni kitendo cha kumfanya mtu aliyekuwa amekufa kuwa hai tena.

Ndugu

Hapa inamaanisha Wakristo, kwa kujumuisha wanaume na wanawake wote, kwa kuwa waumini wote ndani ya Kristo ni washirika wa familia moja, na Mungu ndiye Baba yao wa mbinguni.

Galatians 1:3

kwa dhambi zetu

"dhambi" huwakilisha hukumu ya dhambi. "kuchukua hukumu tuliyostahili kwa sababu ya dhambi zetu"

ili kwamba atukomboe na nyakati hizi za uovu

Hapa neno, "Nyakati...hizi" huwakilisha nguvu zinazotenda kazi katika nyakati husika. "ili kwamba atuweke huru kutoka katika kazi za nguvu ya uovu ndani ya ulimwengu wa leo"

Mungu wetu na Baba

Hii inarejeleaa kwa " Mungu Baba yetu." Ni Mungu wetu na Baba yetu.

Galatians 1:6

Sentensi Unganishi:

Paulo anatoa sababu yake ya kuandika barua hii-anawakumbusha kuendelea kuielewa injili.

Ninashangaa

"Ninashangazwa" au "Nimeshitushwa." Paulo alisikitishwa na mambo haya waliyokuwa wanayafanya.

kwamba mmegeuka haraka sana kutoka kwake... na kwenda kwenye injili nyingine

Maana nyingine zaweza kuwa ni 1) " Mmeacha kwa haraka sana kumtumaini Yeye au 2) "mmeacha kwa haraka sana kuwa waaminifu kwake."

Yeye aliyewaita

"Mungu, aliyewaita ninyi"

kuitwa

Hapa inamanisha Mungu amewateua or kuwachagua watu kuwa watoto wake, kumtumikia na kuutangaza wa ujumbe wa wokovu kupitia kwa Yesu.

kwa neema ya Kristo

" kwa sababu ya neema ya Krsto" au "kwa sababu ya dhabihu ya neema ya Kristo"

Mnageukia injili nyingine

Mnaamini injili nyingine

watu

watu wote au binadamu

Galatians 1:8

anapaswa kutangaza

Hii inaelezea kitu ambacho hakijatokea na hakipaswi kutokea. "wangetangaza" au "walipaswa kutangaza"

tofauti na ile

"tofauti na injili" au "tofauti na ujumbe"

na alaaniwe

"Mungu anapaswa kumwadhibu mtu yule milele yote." na kama lugha yako ina neno au njia inayotumika kutoa laana kwa mtu, unaweza kutumia hiyo.

Kwani sasa hivi ninatafuta uthibitisho wa watu au Mungu? Ninatafuta kuwafurahisha wanadamu?

Maswali haya hutarajia jibu ambalo ni " hapana" Hii ni sawa na kusema "sitafuti kukubaliwa na wanadamu, bali ninatafuta kukubaliwa na Mungu. sitafuti kuwafurahisha wanadamu."

Kama ninaendelea kujaribu kuwafurahisha wanadamu, mimi sio mtumishi wa Kristo

Neno 'kama' linaonesha ukweli kuwa "mimi siwafurahishi wanadamu, mimi ni mtumishi wa Kristo." au " kama ningekuwa bado naendelea kuwafurahisha wanadamu, basi nisingekuwa mtumishi wa Mungu

Galatians 1:11

Sentensi Unganishi

Paulo anaeleza kuwa hakujifunza injili kutoka kwa wengine; alijifunza kutoka kwa Yesu Kristo.

Ndugu

Hapa inamaanisha Wakristo, kwa kujumuisha wanaume na wanawake wote, kwa kuwa waumini wote ndani ya Kristo ni washirika wa familia moja, na Mungu ndiye Baba yao wa mbinguni.

haitokani na watu (si injili ya watu)

kwa kutumia maneno haya, Paulo hasemi kuwa Yesu Kristo mwenyewe si mwanadamu. kwa sababu Kristo ni mtu na ni Mungu, ingawa Yeye si mwanadamu mwenye dhambi. Paulo anaandika juu ya kule injili ilikotoka, kwamba haikutoka kwa watu wenye dhambi, bali ilitoka kwa Yesu Kristo.

kilikuwa ni kwa ufunuo wa Yesu Kristo kwangu

Maana zinazokubalika ni 1) Yesu Kristo mwenyewe aliifunua injili kwangu 2)Mungu alinifanya mimi niijue injili wakati aliponionesha jinsi Yesu Kristo alivyo.

Galatians 1:13

Maisha ya nyuma

"Tabia katika kipindi fulani" au " maisha ya kipindi kilichopita" au " maisha ya mwanzo"

NIlikuwa nimeendelea

Hii ni sitiari ( lugha ya picha) inayoonesha jinsi Paulo alivyokuwa mbele ya wayahudi wengine wa umri wake katika kusudi lao la kuwa wayahudi kamili.

wale wenye umri kama wangu

"Wayahudi wenye umri sawa na wa wangu"

baba

"mababu", au "wazazi wa zamani"

Galatians 1:15

Aliniita kupitia neema yake

Maana zinazokubalika ni 1)"Mungu aliniita kumtumikia kwa sababu Yeye ni wa neema" au 2) " Aliniita kwa njia ya neema yake."

kumdhihirisha Mwanawe ndani yangu

Maana zinazokubalika 1)" kuniruhusu mimi nimjue Mwana wake" 2) "Ulimwengu umwone Yesu Mwana wa Mungu kupitia kwangu."

Mwana

Hili ni jina muhimu la Yesu, Mwana wa Mungu

kumtangaza Yeye

Kumtangaza kuwa Yeye ni Mwana wa Mungu" au "kuhubiri habari njema kuhusu Mwana wa Mungu"

Wala sikutafuta ushauri wa mwili na damu

Haya maelezo yanamaanisha kuzungumza na watu wengine. AT: " kuwaomba watu wanisaidie kuelewa ujumbe."

kupanda

AT: "Kusafiri" Mji wa Yerusalem ulikuwa katika mkoa ulikuwa na milima mingi, ambayo ilimlazimu mtu kupanda milima mingi ili kufika huko, na hivyo ilikuwa kawaida kueleza kitendo cha kusafiri kwenda Yerusalemu kama "kupanda kwenda Yerusalemu."

Galatians 1:18

Lakini sikuona mitume wengine isipokuwa Yakobo

Vikanushi viwili vinatilia mkazo kwamba Paulo alimwona mtume Yakobo tu. AT: Mtume pekee niliyemwona ni Yakobo."

Mbele za Mungu

Paulo anawataka Wagalatia kuelewa kuwa Paulo alikuwa amedhamiria kweli na kwamba Mungu husikia kile anachokisema na kuwa atahukumiwa kama hatausema ukweli.

Tazama, mbele za Mungu, sidanganyi kwa kile niandikacho kwenu

Paulo anatumia msemo huu kuweka mkazo kuwa anausema ukweli. AT: " katika ujumbe huu ninaowaandikia, Siwadanganyi" au " ninasema ukweli katika mambo niliyowaandikia ."

Galatians 1:21

Mikoa ya

"Sehemu ya ulimwengu inayoitwa..."

Walikuwa wakisikia tu

"Bali walikuwa wakijua tu kile wachokisikia kwa wengine kunihusu mimi"

Sikuwa najulikana kwa macho kwa makanisa ya Uyahudi yale yaliyokuwa katika Kristo,

"Hakuna mtu yeyote ambaye alishawahi kukutana nami miongoni mwa makanisa ya Uyahudi yaliyokuwa katika Kristo."

Galatians 2

Wagalatia 02 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Paulo anaendelea kutetea injili ya kweli. Hii ilianza katika Wagalatia 1:11.

Dhana maalum katika sura hii

Uhuru na utumwa

Katika barua hii, Paulo anatofautisha uhuru na utumwa. Mkristo ana uhuru katika Kristo kufanya mambo mengi tofauti. Lakini Mkristo ambaye anajaribu kufuata sheria ya Musa anahitaji kufuata sheria nzima. Paulo anaelezea kwamba kujaribu kufuata sheria ni kama aina ya utumwa. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lawofmoses)

hangamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Siibatili neema ya Mungu"

Paulo anafundisha kwamba, ikiwa Mkristo anajaribu kufuata sheria ya Musa, haelewi neema ambayo Mungu amemwonyesha. Hii ni kosa la msingi. Lakini Paulo anatumia maneno "Siibatili neema ya Mungu" kama aina ya hali ya mawazo. Shabaha ya neno hili inaweza kuonekana kama, "Ikiwa ungeweza kuokolewa kwa kufuata sheria, basi hiyo ingeweza kupuuza neema ya Mungu." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#grace and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-hypo)

<< | >>

Galatians 2:1

Sentense Unganishi

Paulo anaendelea kuwapa historia ya jinsi alivyojifunza injili kutoka kwa Mungu, na siyo kwa mitume.

Alienda

"Alisafiri" Yerusalemu ilikuwa katika nchi ya vilima. Wayahudi pia waliutazama Yerusalemu kama sehemu ya duniani iliyokaribu na mbinguni, hivyo Paulo inawezekana alikuwa akizungumza kwa mfano, au alikuwa akionesha ugumu, kupanda na kusafiri kufika Yerusalemu.

wale waliosemekana kuwa viongozi muhimu

Hawa ni "viongozi muhimu miongoni mwa waumini"

Sikukimbii, au nilikuwa nimekimbia bure

Paulo anatumia neno kukimbia kama lugha ya picha kumaanisha kazi. Na alitumia vikanushi viwili kukazia kuwa kazi aliyokwisha kuifanya ili na faida. AT: "Nilikuwa ninafanya, au nilifanya kazi inayofaa."

kwa bure

"kwa bila faida" au "bila kitu "

Galatians 2:3

Ndugu wa uongo waliotumwa kwa siri

"Watu waliokuja kanisani wakijifanya kuwa ni Wakristo' au watu waliokuja miongoni mwetu wakijifanya kuwa ni wakristo"

Kutahiriwa

Neno hili laweza kuelezwa kwa muundo tendaji. AT " kuwa na mtu wa kumtahiri."

Peleleza uhuru

Hii ina maanisha kuwatazama watu kwa siri ili kuona wanavyoishi katika uhuru.

Uhuru

"uhuru" hali ya kutokuwa chini ya...au utawala wa ..."

Walitaka

Kama: "Wapelelezi hawa walitamani" au "Ndugu hawa wa uongo walitaka"

Kutufanya kuwa watumwa wa sheria

"Kutufanya kuwa watumwa wa sheria." Paulo anazungumzia kuhusu kuwalazimisha kufuata desturi za kiyahudi kama zilivyoamriwa katika sheria. Analizungumzia jambo hili kama ni utumwa. Jambo muhimu la kidesturi hapa ni tohara. "kutulazimisha kutii sheria"

kujitoa katika utii

"kutii" au "kusikia"

Galatians 2:6

Hawakuchangia chochote kwangu

Neno 'kwangu' linawakilisha kile ambacho Paulo alikuwa akifundisha. "halikuongeza chochote kwa kile ninachofundisha" au " hawakuniambia niongeze kitu chochote kwa kile ninachofundisha."

Badala yake

"kinyume"

Nimeaminiwa

Neno hili laweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Mungu ameniamini mimi."

Galatians 2:9

Kujenga kanisa

Ni watu waliwaofundisha watu kuhusu Yesu na kuwashawishi wamwamini Yesu.

Neema niliyopewa mimi

"kwamba Mungu amekuwa mwema kwangu"

kutupokea....mkono wa kulia wa ushirika

"Waliwakaribisha...kama watendakazi wenzao" au "waliwakaribisha...kwa heshima"

Mkono wa kulia

"Mikono yao ya kuume"

Kuwakumbuka masikini

"kushughulikia au kujali mahitaji ya masikini"

Galatians 2:11

Nilipingana waziwazi ( usoni pake)

Maneno "kwa usoni pake" ni lugha ya picha likimaanisha "mahali atakapoweza kuona na kusikia." "Nilikabiliana naye" au "Niliyakosoa matendo yake"

Kabla

Katika uhusiano na wakati/muda

Aliacha

"Aliacha kula pamoja nao"

Alikuwa anawaogopa watu wale

"Alikuwa na hofu na watu hawa waliotaka tohara wangemhukumu kwamba alikuwa akifanya kitu kibaya" au "aliogopa kwamba watu hawa wangemlaumu kwa kufanya jambo fulani baya." kimakosa"

Watu waliotaka tohara

Wayahudi waliokuwa Wakristo, lakini walilazimisha kwamba wale waliomwamini Kristo wanapaswa kuishi kwa kufuata desturi za Kiyahudi.

Kuweka mbali kutoka

"kukaa mbali kutoka" au kuepukwa"

Galatians 2:13

hawafuati injili ya kweli

"Walikuwa wanaishi kama watu ambao hawajaiamini Injili" or " walikuwa wanaishi kana kwamba hawaiamini injili"

Kwa jinsi gani mnaweza kuwalazimisha Watu wa mataifa kuishi kama Wayahudi?

Hili swali linaonesha hali ya kukemea na linaweza kutafsiriwa kama, "mnakosea kuwalazimisha wamataifa kuishi kama Wayahudi." Neno "wewe" linamrejelea Petro na liko katika umoja.

lazimisha

Maana zinakubalika: 1) kulazimisha kwa kutumia maneno or 2) Kushawishi.

Galatians 2:15

Sentensi Unganishi:

Paulo anawaambia waumini kwamba Wayahudi wanaojua sheria na Wamataifa ambao hawaijui sheria, wameokolewa kwa imani peke yake ndani ya Kristo na siyo kwa kutunza sheria.

si watu wa mataifa wenye dhambi

"siyo wale watu wa mataifa ambao wayahudi huwaita wenye dhambi"

Tulikuja katika imani ndani ya Kristo Yesu

"Tuliamini katika Kristo Yesu"

sisi

Huenda pengine hii inamrejelea Paulo na wengine, na si Wagalatia.

hakuna mwili

Neno mwili limetumika kuwakilisha mtu yaani "hakuna mtu"

Galatians 2:17

Lakini kama tunapomtafuta kuhesabia haki ndani ya Kristo

Hii inamaanisha kwamba tumehesabiwa haki kwasababu tumeungana na Kristo na kuhesabiwa haki kwetu kwa njia ya Kristo.

tunajikuta sisi wenyewe pia kuwa wenye dhambi

Maneno "tunajikuta wenye dhambi" yanatilia mkazo kuwa kwa kweli sisi ni wenye dhambi.

sivyo hivyo! La hasha

"Bila shaka hiyo siyo kweli!" Maelezo haya yanatupa jibu hasi kwa swali lililotangulia, Je Yesu alifanyika mtumwa wa dhambi? Unaweza kuwa na maelezo yenye maana sawa katika lugha yako ambayo unaweza kuyatumia hapa.

Galatians 2:20

Mwana wa Mungu

Hili ni jina la muhimu la Yesu

Siikani neema

Paulo anatumia neno hasi katika kutilia mkazo wa ukweli chanya. "ninahakikisha uthamani wa..."

kama haki ingeweza kupatikana kwa.... basi Kristo asingekufa

Paulo anaelezea hali ambayo haipo, haitatokea. "lakini kama haki haipo....basi Kristo hakufa"

kama haki ilikuwepo kupitia sheria, basi Kristo angelikuwa amekufa bure

"kama mtu angeweza kuwa mwenye haki kwa kushika sheria"

angelikuwa amekufa bure

"Kristo angekuwa hajafanya chochote kwa kufa kwake"

Galatians 3

Wagalatia 03 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Usawa katika Kristo

Wakristo wote wameungana kwa usawa na Kristo. Wala uzazi, wala jinsia, wala cheo, vyote havijalishi. Wote wako sawa na wenzake. Wote wako sawa machoni pa Mungu.

Mfano muhimu ya matamshi katika sura hii

Maswali ya uhuishaji

Paulo hutumia maswali tofauti mengi ya uhuishaji katika sura hii. Anayatumia kuwashawishi Wagalatia juu ya dhambi zao. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-rquestion and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Mwili

Hili ni suala ngumu. "Mwili" inaweza kuwa mfano ya asili yetu ya dhambi. Paulo hafundishi kwamba sehemu ya kimwili ya mwanadamu ni ya dhambi. "Mwili" hutumiwa katika sura hii kutofautisha na yale ambayo ni ya kiroho. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#flesh)

"Wale wa imani ni watoto wa Abrahamu"

Wasomi wamegawanyika juu ya maana ya maneno haya. Baadhi yao wanaamini kama Wakristo wanarithi ahadi ambazo Mungu alimpa Abrahamu, kwa hiyo Wakristo wanachukua nafasi ya wazao wa Israeli. Wengine wanaamini kama Wakristo hufuata Abrahamu kiroho, lakini hawarithi ahadi ambazo Mung alimpa Abrahamu. Kwa kuzingatia mafundisho mengine ya Paulo na muktadha hapa, Labda Paulo anaandika hivi kuhusu Wakristo wa Kiyahudi na wa Mataifa walio na imani sawa na Abrahamu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#spirit and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

<< | >>

Galatians 3:1

Sentensi unganishi:

Paulo anawakumbusha waumini wa Galatia kwamba Mungu aliwapa Roho wa Mungu wakati walipoamini injili kwa imani, siyo kwa matendo yao ya kushika sheria

Maelezo ya jumla

Paulo anawakemea Wagalatia kwa kuwauliza swali la uchokozi na Kejeli

Nani amewawekea uchawi?

Paulo anatumia swali la uchokozi kwa kusema kuw Wagalatia wanatenda kama kuna ameweka laana au uchawi. Haamini kwa hakika kwamba mtu mmoja ameweka uchawi kwao. "Mnaenenda kana kwamba mtu amewawekea uchawi"

Mimi nataka tu kufahamu hili kutoka kwenu

Huu ni mwendelezo wa hoja kutoka mstari 1. Paulo anajua majibu ya maswali anayoyauliza.

Mlimpokea Roho kwa matendo ya sheria au kwa imani ambayo mliisikia?

"Mlimpokea Roho, si kwa matendo kama sheria isemavyo, lakini kwa kuamini kile mlichosikia."

Je ninyi ni wajinga?

Swali hili lenye jibu linaonesha mshangao wa Paulo na hata hasira yake kwa Wagalatia Wagalatia ni wajinga. "Ninyi (wingi) mu wajinga kweli!" .

katika mwili

Neno mwili ni lugha ya picha linalomaanisha juhudi. "kwa juhudi zako" au "kwa kazi yako mwenyewe."

Galatians 3:4

Je mmeteseka kwa mambo mengi bure?

Paulo anauliza swali hili kuwakumbusha Wagalatia kwamba wakati walikuwa wakiteseka, wal wakiamini kuwa watakakalenye jibu kuwakumipoamibusha Wagalatia kwa maisha magumu waliyoteswa nayo.

Mmteseka sana na mambo mengi kwa bure

inaweza kuelezwa kwa uwazi kuwa waliteseka kwa mambo haya kwasababu ya watu waliopinga imani yao ndani ya Yesu. "Je umeteseka bure kwa mambo mengi kwa ajili ya ya wale wanaowapinga nyie kwasababu ya imani yenu katika Kristo." "Mlimwamini Yesu, na mmeteseka kwa mambo mengi kutoka kwa wale wanaomping Kristo." "Je imani na mateso yenu ni bure"

kwa bure

"isiyofaa" au "pasipo na matumaini ya kupokea kitu chochote"

kama kweli ilikuwa bure?

Maana zinazokubalika 1) Paulo anatumia swali hill kuwaonya ili kazi yao isiwe ya bure. "Msiifanye kazi isiyo na faida au msiache kuamini katika Yesu Kristo na mkayacha mateso yenu yakawa ya bure." 2) Paulo anatumia swali hili kuwaaminisha kuwa mateso yao si bure. "kwa kweli si bure."

Je yeye atoaye Roho kwenu na kutenda matendo ya nguvu kati yenu hufanya kwa matendo ya sheria au kwa kusikia pamoja na imani?

Paulo anatumia tena swali kuwakumbusha Wagalatia jinsi watu wanavyompokea Roho. "Hafanyi hivyo kwa matendo ya sheria, anafany kwa kusikia pamoja na imani."

kwa matendo ya sheria

Hii inawakilisha watu wanaofanya matendo yatokanayo na matakwa ya sheria. "Kwasababu unafanya yale unayoagizwa na sheria kufanya."

kusikia kwa imani

Lugha yako yaweza kuhitaji kuwa na maneno ya wazi kuelezea kile watu walichokisikia kutoka kwa mtu wanayemwamini. "kwasababu uliusikia ujumbe na kumwamini Yesu" au " kwasababu uliusikiliza ujumbe na kumtumaini Yesu."

Galatians 3:6

Sentensi unganishi:

Paulo anawakumbusha Waumini wa Galatia kwamba hata Ibrahimu aliipokea haki kwa imani na siyo kwa sheria.

ilihesabiwa kwake mwenye haki

Mungu aliiona imani ya Ibrahimu katika Mungu, hivyo Mungu alimhesabia Ibrahimu haki.

ambao wanaamini ( wenye imani)

"watu walioamini" Maana ya nomino 'imani' laweza kuelezwa kwa kitenzi 'kuamini" "wale wanaoamini"

watoto wa Ibrahimu

inawakilisha watu wale ambao Mungu huwatazama kama alivyomtazama Ibrahimu. "Mwenye haki kwa namna moja kama ya Ibrahimu."

tangulia kuwaona

Kwa sababu Mungu alimwahidi Ibrahimu na ikaandikwa kabla ahadi hiyo kuja kupitia Kristo, maandiko ni kama mtu ambaye huona muda ujao kabla ya kutokea. "Ilitabiriwa" au " kuona kitu kabla hakijatokea."

katika wewe

"Kwa sababu ya kile umekwisha tenda" au "kwasababu nimekwisha kukubariki" Neno wewe humrejelea Ibrahimu katika umoja.

mataifa yote

"makundi ya watu wote duniani". Mungu alikuwa akielezea kwa mkazo kwamba alikuwa hapendelei wayahudi tu, kundi alilolichagua. Mpango wake wa wokovu ulikuwa kwa wote wayahudu na wasio wayahudi.

Galatians 3:10

Wale ambao wanategemea matendo ya sheria wako chini ya laana

Kuwa chini ya laana inamaanisha kuwa umelaaniwa. Hapa inaonesha kuwa ni kuhukumiwa milele. " Wale wanaotegemea matendo ya sheria wamelaaniwa" au "Mungu atawahukumu hukumu ya milele wale ambao wanategemea matendo ya sheria"

Sasa ni wazi kwamba Mungu huhesabia

Kile kilicho wazi huelezwa dhahiri. "Maandiko yako wazi" au "maandiko yanafundisha wazi wazi."

Mungu hamhesabii haki hata mmoja kwa sheria,

kifungu hiki cha maneno kinaweza kuelezwa kwa kitenzi kitendaji. "Mungu hahesabu haki kwa mtu hata mmoja kwa njia ya sheria"

Mungu hamhesabii haki hata mmoja kwa sheria,

Paulo anasahihisha imani yao kwamba kama wangeitii sheria, Mungu angewahesabia haki. "Hakuna hata mmoja ambaye anaweza kuhesabiwa haki mbele za Mungu kwa kutii sheria" au "Mungu hamhesabii mtu haki kwa utiifu wao wa sheria."

wenye haki

Hii inarejelea watu wenye haki. "Watu wenye haki" au "Watu wale ambao Mungu huwaona ni wenye haki"

matendo ya sheria

"Lazima kufanya yote yanayosemwa na sheria "

ishi kwa sheria

Maanza zinazokubalika 1) Ni lazima kutii "ishi kulingana na" au "Jinyenyekeze kwa" au "salia mwaminifu kwa" au "tii" au "tekeleza"

wataishi kwa sheria

Maana zinazowezekana ni: 1) "lazima kuzitii sheria zote" 2) atahukumiwa kwa sababu ya uwezo wake wa kuishi kama vile sheria zinamwagiza kutenda"

Galatians 3:13

Sentensi unganishi:

Paulo anawakumbusha waumini hawa tena kwamba kutunza sheria kusingemwokoa mtu na kwamba sheria hazikuweza kuongeza hali mpya kwenye ahadi ya imani iliyotolewa kwa Ibrahimu.

kutoka laana ya sheria

Nomino "laana" inaweza kuelezwa kwa kitenzi "laani" kutoka katika laana ya sheria" au " Kutoka katika laana ya kutokutii sheria."

alikuwa laana kwa ajili yetu

Nomino "laana" inaweza kuelezwa kwa kitenzi "laani" "Kwa kulaaniwa kwa ajili yetu" au "Wakati Mungu alipomlaani badala yetu."

kutoka katika laana ya sheria wakati alipofanyika laana kwa ajili yetu......, "Amelaaniwa kila mtu ...

Laana katika muktadha huu inawakilisha hukumu. "kutoka katika hukumu ya sheria...alihukumia badala yetu ....amehukumia mtu yeyote"

kuangikwa juu ya mti

Paulo alitarajia hadhira yake kuelewa kwamba alikuwa akielezea kuangikwa kwa Yesu juu ya msalaba.

yaweza

"yawezekana" au "ita"

sisi

Neno 'sisi' linamjuisha Paulo pamoja na watu watakaosoma waraka huu.

Galatians 3:15

ndugu

Hapa inamaanisha Wakristo, kwa kujumuisha wanaume na wanawake wote, kwa kuwa waumini wote ndani ya Kristo ni washirika wa familia moja, na Mungu ndiye Baba yao wa mbinguni.

lugha za kibinadamu

"kama mtu" au "mambo ambayo watu wengi huyaelewa"

Sasa

Paulo anaonesha kuwa amejadili kanuni ya jumla na sasa anatambulisha jambo la kipekee.

kumaanisha wengi

"kumaanisha uzao wa mwingi"

kwa kizazi chako

Neno "chako" ni umoja, na unarejelea kwa mtu mmoja mahususi, ambaye ni uzao wa Ibrahimu ( na uzao huo unaainishwa kama "Kristo")

Galatians 3:17

Kwa kuwa kama urithi ungelikuja kwa njia ya sheria, usingekuwa tena umekuja kwa njia ya ahadi

Paulo anaongelea hali ambayo haipo ili kutia makazo kwamba urithi unakuja tu kwa njia ya ahadi. " Urithi unakuja kwetu kwa njia ya ahadi kwa sababu hatukuweza kutunza matakwa ya sheria za Mungu"

urithi

Ni kupokea kile ambacho Mungu kwa maneno awewaahidi waumini kama ulivyo urithi wa mali na utajiri kutoka kwa mwana familia,na baraka za milele na ukombozi.

Galatians 3:19

Sentensi unganishi:

Paulo anawaambia waumini wa Galatia sababu ya Mungu kuwapa sheria.

Kwanini tena sheria ilitolewa?

Paulo anatua swali katika kutambulisha mada ijayo anayotaka kuijadili. inaweza pia kutafsiriwa kama maelezo. "nitawaambia nini makusudi ya sheria. au "acheni niwaambie kwa kwanini Mungu aliwapa sheria?

Iliongezwa

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. "Mungu aliiongeza" au"Mungu aliongeza sheria"

Sheria iliwekwa katika shinikizo kupitia malaika kwa mkono wa mpatanishi

Hii inaweza kufasiriwa katika muundo tendaji. Mungu aliweka sheria kwa msaada wa malaika , na mpatanishi akaipisha au kuirasimisha"

Mpatanishi

mwakilishi

mpatanishi anaashiria zaidi ya mtu mmoja, lakini Mungu ni mmoja

Mungu alimwahidi Ibrahimu pasipo mpatanishi, lakini alimpa Musa sheria kupitia kwa mpatanishi. kutokana na hicho, wasomaji wa waraka wa Paulo walifikiri kwamaba sheria imeifanya ahadi isiwe na umuhimu. Paulo anaeleza kile ambacho wasomaji wake wanaweza kuwa wanafikiria. Naye atatoa maelezo yake katika mistari inayofuata.

Galatians 3:21

Maelezo ya jumla

Neno "sisi" linarejelea wakristo wote.

badala ya

"kinyume cha" au "katika mgongano na"

kama sheria ilikuwa imetolewa ilikuwa na uwezo wa kuleta uzima,

Hii inaweza kuelezwa kwa muundo tendaji, na nomino dhahania "maisha" inaweza kutafsiriwa na kitenzi "ishi" "Kama Mungu angekuwa ametoa sheria inayowawezesha wote walioishika kuishi, tungekuwa wenye haki kwa kushika sheria"

andiko limefunga mambo yote chini ya dhambi. Mungu alifanya hivi ili kwamba ahadi yake ya kutuokoa sisi kwa imani katika Yesu Kristo iweze kupatikana kwa wale wanaoamini.

Maana nyingine zinazowezekana ni: 1) "Kwa sababu wote tumetenda dhambi, Mungu aliweka mambo yote chini ya uongozi wa sheria kama kuwaweka katika kifungo, ili kwamba kile alichoahidi kwa hao ambao wenye imani katika Kristo Yesu aweze kuwapatia ambao wameamini" 2) "kwasababu tunatenda dhambi, Mungu ameweka mambo yote katika kifungo. Alifanya hivi kwasababu ya kile alichokiahidi katika Kristo Yesu awape wale wanaoamini"

maandiko

Paulo anayaona maandiko kama alikuwaa ni mtu anaongea na Mungu, ambaye aliyaandika maandiko "Mungu"

Galatians 3:23

Sentensi unganishi:

Paulo anawakumbushaWagalatia wote kwamba waumini wako huru katika familia ya Mungu, si watumwa chini ya sheria.

tulikuwa tumefungwa na kuwa chini ya sheria

kifungu hiki cha maneno kinaweza kuelezwa kwa kutumia muundo tenda. "sheria ilitufunga na tukawa kifunguni." au "sheria ilitunga gerezani."

tulikuwa tumefungwa na kuwa chini ya sheria

Kwa namna ambavyo sheria zilituongoza ni kana kwamba sheria alikuwa mlinzi wa gereza aliyetushikilia. "sheria zilituongoza mfano wa mlinzi wa gereza"

hadi ufunuo wa imani

Kifungu hiki cha maneno kinaweza kwa muundo tendaji. "mpaka Mungu alipodhihirisha kwamba huwahesabia wale wote wanaomtumaini Kristo" au "mpaka Mungu alipofunua kwamba huhesabia wale wote wenye imani katika Kristo"

mwangalizi

Neno hili ni zaidi ya "mtu yule anayemwangalia mtoto." huyu alikuwa ni Mtumwa aliyewajibika na usimamizi wa kanuni na mwenendo uliotolewa na wazazi, na ambaye alitakiwa kutoa taarifa kwa wazazi juu ya matendo ya mtoto.

mpaka Kristo alipokuja

"mpaka ule muda ambao Kristo alikuja"

ili tuweze kuhesabiwa haki

Mungu alikusudia kutuhesabia haki kabla ya ujio wa Yesu. Yesu alipokuja , alitekeleza kusudi lake la kutuhesabia haki. Inaweza kuelezwa kwa muundo tenda" "Kwamba Mungu angetutangaza kuwa wenye haki"

Galatians 3:27

wenyewe mmejivika Kristo

Maana zinazowezekana ni 1) "mmekuwa sawa kama na ubinadamu wa Kristo" au 2) " mmekuwa na mahusiano sawa na Mungu kama ya Kristo

Hakuna Myahudi wala Myunani, mtumwa wala huru, mwanaume wala mwanamke,

Mungu anaona kuwa hakuna utofauti kati ya wayahudi na wayunani, mtumwa na mtu huru, mwanamme na mwanamke.

warithi

Watu ambao Mungu amewapa ahadi wanaongelewa kama warithi wa mali na utajiri kutoka kwa mwana familia.

Galatians 4

Wagalatia 04 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri huweka kila mstari wa mashairi upande wa kulia zaidi kuliko maandiko yote ili iwe rahisi kusoma. ULB inafanya hivi kwa mstari wa 27, ambao umenukuliwa kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

Uwana

Uwana ni suala ngumu. Wasomi wana maoni mengi juu ya uwana wa Israeli. Paulo anatumia uwana wa kufundisha jinsi kuwa chini ya sheria hutofautiana na kuwa huru katika Kristo. Si wote wa uzao wa Abrahamu ambao ni wao waliorithi ahadi za Mungu kwake. Uzazi wake tu kupitia Isaka na Yakobo walirithi ahadi. Na Mungu huweka katika familia yake wale tu wanaomfuata Abrahamu kiroho kupitia imani. Wao ni watoto wa Mungu wenye urithi. Paulo anawaita "watoto wa ahadi." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#inherit, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#promise, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#spirit and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#adoption)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Abba, Baba

"Abba" ni neno la Kiaramu. Katika Israeli ya kale, watu walitumia kwa usawa kutaja baba zao. Paulo "hufasiri" sauti zake kwa kuandika kwa herufi za Kigiriki. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-transliterate)

<< | >>

Galatians 4:1

Kauli Unganishi

Paulo anazidi kuwakumbusha wakristo wa Galatia kwamba Kristo alikuja kukomboa wale waliokuwa chini ya sheria, na kuwafanya wasiwe watumwa tena bali wana.

hakuna utofauti

"kuwa sawa na "

waangalizi

Watu wenye wajibu wa kisheria kuangalia watoto

wadhamini

ni watu wanaoaminiwa na wengine kutunza vitu vyenye thamani

Galatians 4:3

Maelezo ya jumla

neno 'sisi' linarejelea Wakristo wote, na wasomaji wa nyaraka wa Paulo

Kanuni za kwanza za ulimwengu

Maana zinazokubalika ni 1) inarejelea sheria na kanuni za kimaadili za ulimwengu 2) inarejelea nguvu za kiroho, ambazo baadhi ya watu wanadhani zinatawala kile kinachotokea duniani.

kukomboa

Paulo anatumia sitiari ya Mtu aliyenunua tena mali zake alizozipoteza au kumnunulia uhuru mtumwa. hii ni picha ya Yesu aliyelipa deni la dhambi za watu kwa kufa pale msalabani.

Mwana

Hili ni jina muhimu sana la Yesu, Mwana wa Mungu.

Galatians 4:6

ninyi ni wana.....si watumwa tne bali wana

Hapa Paulo anatumia neno la watoto wa kiume kwasababu ya jambo la Urithi.katika utamaduni wa wasomaji wake, urithi mara nyingi, lakini si mara zote, ulikuwa ni wa watoto wa kiume tu. Paulo alikuwa hapendelei watoto wa kiume na kuwatenga watoto wa kike hapa.

Mungu alimtuma Roho wa mwanawe ndani ya mioyo yetu, Roho aitaye, "Abba, Baba."

Mungu Baba amemtuma Roho wa Mwana wa Mungu katika mioyo ya waumini. Sasa wanajua kuwa anawapenda wakati wote kama baba mwema anavyowapenda watoto wake.

Kutumwa kwa Roho wa Mwanawe ndani ya mioyo yetu.

Neno moyo limetumika kuwakilisha sehemu ya mtu inayofikiria na kuhisi. "kutuma Roho ya Mwana wake kutuonyesha jinsi ya kufikiri na kutenda"

Mwana

Hiki ni jina muhimu la Yesu, Mwana wa Mungu.

Anayeita

Roho ndiye anayeita

Abba, baba

Hii ni namna ya mtoto anavyojieleza kwa baba yake katika lugha aliyokuwa akiitumia Paulo, ingawa si katika lugha iliyokuwa ikitumiwa na wasomaji wa Galatia. Ili kutunza lugha hiyo ngeni ni vema kulitafasiri kama linavyosikika kama "Abba" ikiwa lugha yako inavyoruhusu.

wewe si mtumwa tena bali ni mwana

Paulo anawazungumzia wasomaji wake kana kwamba ni mtu mmoja, 'wewe' huu ni umoja.

warithi

Watu ambao Mungu amewapa ahadi wanaongelewa kama warithi wa mali na utajiri kutoka kwa mwana familia

Galatians 4:8

Sentense unganishi

Paulo anawakumbusha tena wasomaji wake kuwa wanajaribu tena kuishi chini ya sheria badala ya kuishi kwa imani.

Maelezo ya jumla

Hapa Paulo anaendelea kuwakemea Wagalatia kwa kuwauliza maswali ya kejeli, yasiyohitaji majibu

Mnajulikana na Mungu

inaweza pia kuelezwa kwa muundo tendaji kama "Mungu anawajua"

kwa nini mnarejea tena... kanuni?

Hili swali la kwanza kati ya maswali mawili yanayo na majibu ndani yake. "Kuwa msirejee tena nyuma katika kanuni za awali."

Kanuni za awali

Maana zinazokubalika ni 1) inarejelea sheria na kanuni za kimaadili za ulimwengu 2) inarejelea nguvu za kiroho, ambazo baadhi ya watu wanadhani zinatawala kile kinachotokea duniani.

Mnataka kuwa watumwa tena?

Swali hili laweza kutafsiriwa kama maelezo tu "Hamtakiwi kuw mtumwa tena" au "Inaonyesha kuwa mnataka kuwa watumwa tena."

Galatians 4:10

mnashika kwa uangalifu siku amaalumu, miandamo ya miezi, majira, na miaka

Paulo anazungumzia juu yao kuwa waangalifu katika kusherehekea vipindi/nyakati fulani, wakiamini kuwa kwa kufanya hivyo watakuwa wenye haki. "mko makini katika kusherehekea siku na miandamo ya miezi na majira na miaka"

mnajitaabisha bure

"kuwa katika hali ya kutofaa, "bila mafanikio" au "kukosa faida"

Galatians 4:12

Sentensi unganishi

Paulo anawakumbusha waumini wa Galatia jinsi walivyokuwa wema katkia kumhudumia wakati akiwa pamoja nao, na anawatia moyo kuendelea kumtumaini hata wakati asipokuwa pamoja nao.

Sihi

Neno hili linamaanisha kuomba kwa nguvu. Hili si neno lililotumika kuomba pesa, chakula au kitu kingine chochote cha mahitaji.

Ndugu

Hapa linamaanisha wakristo wote wa kike na wakiume, ndugu walio katika Kristo ni washirika wa familia moja ya kiroho, pamoja na Mungu Baba yao wa mbinguni.

Hamjanitenda kosa

kwa kutumia maneno haya, Paulo anatilia mkazo kwa Wagalatia walihudumia vizuri sana "Mlinitunza vizuri sana", au "mlinitunza kama mlivyopaswa"

Ingawa afya yangu iliwaweka katika jaribu

"Ingawa ilikuwa vigumu kuniona mimi wakati nikiwa mgonjwa"

kudharau

kuchukia sana

Galatians 4:15

Nimekuwa adui kwenu kwa kuwambia ukweli?

Mnaonekana kufikiri kuwa nimekuwa adui yenu kwa kusema ukweli kwenu?

Galatians 4:17

Kwa huruma wanawatafuta...muwafuate...

"kuwashawishi ili muungane pamoja nao. Paulo anaonyesha nia ya walimu wa uongo iliyokuwepo, walionyesha huruma kwa Wagalatia ili wawafuate wao kwa lengo la kuwaondoa kwenye kweli.

kuwatenganisha

"kuwatenganisha ninyi na mimi" au "kuwafanya mwache kuwa waaminifu kwangu"

kwa shauku

Shauku ya Kufanya kile wanachowaambia

Galatians 4:19

Sentensi unganishi

Paulo anawaambia waumini kwamba neema na sheria haziwezi kufanya kazi kwa pamoja.

Watoto wangu wadogo

Hii ni sitiari kurejelea wanafunzi au wafuasi. " Ninyi mlio wanafunzi kwasababu yangu."

Nateseka kwa uchungu mkali kama wa mwanamke azaapo mpaka Kristo aumbike ndani yenu.

Paulo anatumia neno 'uchungu" kama lugha ya picha kuonesha namna alivyojihusisha na Wagalatia. "Niko katika mateso ni kana kwamba nimekuwa mwanamke aliyeshikwa na utungu wa kuwazaa, na nitaendelea kuwa katika mateso mpaka Kristo atakapowatawala maisha yenu kikweli kweli.

Galatians 4:21

Niambieni

Ni hali ya kutaka kuuliza swali au ninataka kuwaambia jambo fulani

Hamsikii sheria isemavyo?

Paulo anatoa utangulizi kwa jambo analokusudia kulisema baadaye. "Mnapaswa kujifunza vile sheria isemavyo" ama "niwaeleze sheria isemavyo"

Galatians 4:24

Sentensi unganishi

Paulo anaanza habari kwa kueleza ukweli kuwa neema na sheria haziwezi kuwa sehemu moja kwa pamoja na kwa wakati mmoja.

Mambo haya yanaweza kuelezwa kwa kutumia mfano,

"Habari hii ya wana wawili ni picha hii ya kile ninachowambieni sasa."

mfano

Mfano ni namna ya kiuandishi uliotumika kutoa maana fulani, mfano; watu na vitu vimetumika kuwakilisha vitu vingine au maana fulani. Katika mfano huu wa Paulo, wanawake wawili wametumika kurejelea aina mbili za maagano 4:21.

Mlima Sinai

Mlima Sinai umetumika kama kiwakilishi cha sheria. Ni mahali Musa alipopokea mbao mbili za sheria kwa ajili ya wana wa Waisrael.

Huzaa watoto ambao ni watumwa

Paulo anaiona sheria kama vile ni mtu. Watu waliochini ya agano la sheria ni watumwa wanaopaswa kuitii sheria.

Fananishwa

Ni mifano yenye kutoa picha ya kuleta maana fulani.

Yuko katika utumwa pamoja na watoto wake

Hajiri ni mtumwa na watoto wake wako utumwani pamoja naye. Yerusalemu ni kama Hajiri na watoto wake ni watumwa pamoja naye.

Galatians 4:26

Huru

Hapa huru inamaanisha hali ya kutofungwa, kutokuwa mtumwa.

Furahi

Changamka, shangilia, kuwa na furaha.

uliye tasa, wewe usiye zaa...... wewe ambaye huna uzoefu wa kuzaa.

Neno hili 'wewe' kwa hapa linamrejelea mwanamke tasa na liko katika hali ya umoja.

Galatians 4:28

Ndugu

Neno linalomaanisha wafuasi wa Kristo wote wa kiume na wa kike. Waumini wote wa Yesu Kristo ni jamii moja na familia moja ya kiroho iko pamoja na Mungu Baba yao wa mbinguni.

watoto wa ahadi

Maana zinazokuballika kwa Wagalatia kuwa watoto wa Mungu ni 1) kwa kuziamini ahadi za Mungu 2) kwasababu Mungu anatenda miujiza katika kutimiza ahadi zake kwa Ibrahimu, kwanza kwa kumpa Ibrahimu mwana na pia kwa kuwafanya Wagalatia watoto wa Ibrahimu na wa Mungu pia.

Kutokana na mwili

Neno hili linafafanua kitendo cha Ibrahimu kuwa Baba wa Ishmael kwa kumtwaa Hajiri kuwa mke wake. "Kwa matendo ya kibinadamu" au 'Kwasababu ya kile watu walichokifanya."

Kutokana na Roho

Kwasababu ya uongozi wa Roho katika kutimiza mapenzi yake.

Galatians 4:30

Ndugu

Neno linalomaanisha wafuasi wa Kristo wote wa kiume na wa kike. Waumini wote wa Yesu Kristo ni jamii moja na familia moja ya kiroho iko pamoja na Mungu Baba yao wa mbinguni.

bali ni wa mwanamke huru

Maneno yaliyoachwa nje yanaweza yakapachikwa hapa "lakini badala yake, sisi ni watoto wa mwanamke huru."

Galatians 5

Wagalatia 05 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Paulo anaendelea kuandika juu ya sheria ya Musa kama kitu kinachomtega mtu au kumfanya mtumwa. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lawofmoses)

Dhana maalum katika sura hii

Tunda la Roho

aneno "tunda la Roho" sio wingi, ingawa huanza orodha ya vitu kadhaa. Watafsiri wanapaswa kuweka fomu ya umoja ikiwezekana. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#fruit)

Mfano muhimu ya matamshi katika sura hii

Mifano

Paulo anatumia mifano kadhaa katika sura hii ili kuonyesha pointi zake na kusaidia kuelezea masuala magumu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Ninyi mmekatwa kutoka kwa Kristo, ninyi mtakaohesabiwa haki na sheria, hamna tena neema."

Wasomi wengine wanafikiri kama Paulo anafundisha kwamba kutahiriwa husababisha mtu kupoteza wokovu wake. Wataalamu wengine wanafikiri kama Paulo anamaanisha kwamba kutii sheria ili kujaribu kupata haki na Mungu utamzuia mtu kuokolewa kwa neema. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#grace)

<< | >>

Galatians 5:1

Sentensi Unganishi

Paulo anatumia mfano kwa kuwakumbusha waumini kutumia uhuru wao katika Kristo kwa sababu sheria yote imekamilika katika kumpenda jirani kama sisi wenyewe.

Ni kwa Uhuru

Tafsiri inahitaji kusisitiza "uhuru" kinyume cha utumwa uliozungumzwa katika mistari iliyotangulia

Ni kwa uhuru ambao Kristo ametuweka sisi huru

"ili kwamba tuweze kuwa kuwa huru maana Kristo ametuweka huru"

simameni imara

kusimama imara hapa inawakilisha hali ya kutobadilika. Hali ya kutobadilika inaweza kuelezwa kwa uwazi. "msikubali hoja za watu wengine wanaowafundisha vitu tofauti" au " dhamirieni kuwa huru"

kama mtakuwa mmetahiriwa

Paulo anatumia neno 'tohara' kama lugha ya mfano au picha kumaanisha dini ya kiyahudi. "Kama mtarudi kwenye Dini ya Kiyahudi"

Galatians 5:3

shuhudia

"tangaza" au "tumika kama shahidi"

kwa kila mtu aliyetahiriwa

Paulo anatumia neno 'tohara' kama kwa kumaanisha hali ya kuwa Myahudi. "kwa kila mtu ambaye amekuwa Myahudi"

wajibika

"amefungwa" au "zuiliwa" au "kufanywa kuwa watumwa"

Ninyi mmetengwa ktoka kwa Kristo

"Ninyi mmekomesha au kusitisha uhusiano wenu na Kristo"

ninyi wote "mnaohesabiwa haki" kwa sheria

Paulo anaongea kwa kinyume hapa. Anafundisha hasa kwamba hakuna Myahudi anayeweza kuhesabiwa haki kwa kufanya matendo yanayotakiwa na sheria. "ninyi wote mnaodhani mnaweza kuhesabiwa haki kwa kufanya matendo yanayotakiwa na sheria" au " ninyi mnataka kuhesabiwa haki kwa njia ya sheria"

Ninyi mmeanguka mbali na neema

Yule anayetoa neema anaweza kuelezwa kwa uwazi zaidi. "Mungu hatawaonesha neema yake kwenu"

Galatians 5:5

Maelezo ya jumla

hapa, neno 'sisi' linarejelea kwa Paulo na wale wanaopinga tohara ya Wakristo. Yeye bila shaka wakiwemo na Wagalatia.

Kwa kuwa

"Hii ni kwa sababu"

kwa imani, tunasubiri tumaini la haki

Maana zinazokubalika ni 1) "Tunasubiri kwa imani tumaini la haki" au 2) "tunasubiri tumaini la haki ambalo linakuja kwa imani."

tunasubiri kwa hamu tumaini la haki

"Tunasubiri kwa uvumilivu na kwa shauku kuwa Mungu atatufanya wenye haki pamoja naye milele, na tunamtarajia kuwa Mungu atafanya hivyo.

kutahiriwa au kutokutahiriwa

maneno ya mfano yakimaanisha kuwa Myahudi or Mmataifa yaani asiye myahudi. "si kwa kuwa myahudi au kutokuwa myahudi"

Ni imani pekee inayofanya kazi kupitia upendo

"Badala ya hiyo, Mungu anajishughulisha na imani yetu katika yeye, ambayo tunaionesha kwa kuwapenda wengine

humaanisha kitu

ina thamani

Mlikuwa mnapiga mbio

"Mlikuwa mnafanya kile mlichofunzwa na Yesu"

Ushawishi wa kufanya hivyo hautoki kwake yeye anayewaita ninyi

"Yule anayewashawishi kufanya hivyo siyo Mungu, anayewaita"

yeye anayewaita

kusudi la kuwaita laweza kuelezwa hapa wazi. "yeye aliyewaita muwe watu wake"

ushawishi

Kumshawishi mtu fulani ni kumfanya mtu huyo abadili kile anachoamini na hivyo kutenda tofauti.

Galatians 5:9

hamtafikiri kwa njia nyingine yoyote

"hamtaamini kitu chochote totauti na kile ninachowaambia"

yeyote yule atakayepotosha atabeba hukumu

" Mungu atamwadhibu mtu huyo anayewapotosha na kuwasumbua"

Anayewapotosha ninyi

"anayesababisha ninyi mkose uhakika wa kipi ni kweli" au "kuinua shida miongoni mwenu"

Yeyote awaye

Maana zinazokubalika ni 1) Paulo hajui majina ya watu wanaowaambia Wagalatia kwamba wanahitaji kutii Sheria ya Musa au 2) Paulo hataki Wagalatia washughulike kujua kama wale wanaowasumbua ni matajiri au maskini au wakubwa au wadogo au wenye au wasio na dini

Galatians 5:11

Ndugu, kama naendelea kutangaza tohara, kwa nini bado ninateswa?

Paulo anaelezea hali ambayo haipo kwa kukazia kuwa watu wanamtesa kwasababu hahubiri watu wawe wayahudi. Hii yaweza pia kuelezwa kwa muundo tendaji. " ndugu mwaweza kuona kuwa siendelei kutangaza habari za tohara kwa sababu wayahudi wananitesa"

Ndugu

"Ndugu." Neno la kiswahili "ndugu" linamaanisha watu wa kike na wa kiume.

Kwa suala hilo kile ambacho ni kizuizi cha msalaba kitaweza kuharibiwa

Paulo anaelezea juu ya hali ambayo haipo ili kukazia kwamba watu wanamtesa kwasababu anahubiri kwamba Mungu huwasamehe watu kwasababu ya kazi ya Yesu juu ya msalaba.

jambo hilo

"kama ningekuwa bado ninasema kwamba watu wanatakiwa kuwa wayahudi"

kizuizi cha msalaba kimeondolewa

msemo huu waweza kuelezwa kwa muundo tenda: kwamba ujumbe kuhusu msalaba hauna kizuizi" au " hakuna kizuizi chochote katika mafundisho ya msalaba yanaweza kuwafanya watu wajikwae."

kizuizi cha msalaba kimeondolewa

kujikwaa inawakilisha hali ya kutenda dhambi, na kizuizi inamaanisha kitu kile kinachowafanya watu watende dhambi. katika jambo hili, dhambi ni kuukataa ukweli wa mafundisho kwamba watu wanatakiwa kuamini kuwa Yesus Kristo alikufa msalabani ili watu wawe na haki mbele za Mungu. "Mafundisho juu ya msalaba yanayowafanya watu kuukataa ukweli yamekwisha kuondolewa"

watajihasi wenyewe

Maana zinazokubalika ni 1) kukata viungo vyao vya kiume ili wawe matowashi au 2) kujikata au kujiondoa wenyewe kutoka katika ushirika wa watu wa Mungu

Galatians 5:13

Kwa kuwa

Paulo anatoa sababu kwa maneno yake yaliyo katika 5:11:

Mmeitwa katika uhuru

kifungu hiki cha maneno chaweza kuelezwa katika muundo tendaji. "Mungu amewaita katika uhuru"

Mungu amewaiteni ninyi kwenye uhuru.

Maana zinazokubalika ni 1) Mungu amewachagua ninyi kuwa watu wake ili kwamba muwe huru au 2) Mungu ameamuru ninyi muwe huru.

Ndugu

Ndugu hurejea kwa wakristo wa " kiume na wa kike"

fursa kwa ajili ya mwili

"nafasi ya kufanya kile kinachoridhisha asili yenu ya dhambi," Hii inarejelea hasa vitu ambavyo vinaleta madhara kwa mtu mwenyewe binafsi au majirani

sheria yote imekamilika katika amri moja

Maana zinazokubalika ni 1) "unaweza kueleza sheria yote katika amri moja, ambayo ni hii" au 2) kwa kutii amri moja, unatii amri zote, na hiyo amri ni hii."

Ni lazima umpende jirani yako kama wewe mwenyewe

maneno "wewe," "yako," na "wewe mwenyewe" yote yako katika umoja

Galatians 5:16

Sentensi unganishi

Paulo anaeleza jinsi Roho anavyo na mamlaka dhidi ya dhambi

tembea kwa kwa Roho

Kutembea ni mfano wa kuishi. "enendeni katika maisha yenu katika nguvu za Roho Mtakatifu" au "ishi maisha yako kwa kumtegemea Roho"

hamtazitimiza tamaa za mwili

"hamatazifanya dhambi ambazo mnataka kuzifanya kwa sababu mko binadamu"

hamko chini ya sheria

Hamuwajibiki kutii sheria ya Musa

Galatians 5:19

matendo ya mwili

Paulo anatumia neno "mwili" kama sitiari au mfano unaowakilishi asili ya mwanadamu."mambo yanayofanywa kama matokeo ya utu wa dhambi ya asili ya mtu"

kurithi

Kupokea kile ambacho Mungu amekwisha kuwaahidi waumini kama kurithi mali na utajiri kutoka kwa mwana familia.

Galatians 5:22

tunda la Roho ni upendo...kiasi

Paulo anatumia sitiari kuonesha kile ambacho watu wanaweza kukiona kwa watu wengine. "Watu ambao wanaongozwa na Roho wataonesha upendo ...kiasi kama vile mti unavyozaa tunda."

tunda la roho

Ni kile ambacho Roho huzalisha"

wameusulibisha mwili pamoja na shauku na tamaa zake mbaya

Paulo anaongelea Wakristo ambao huzuia tamaa mbaya kana kwamba tamaa hizo walikuwa ni watu ambao wakristo walikuwa wakiwaua. "tumeua asili yetu ya dunia pamoja na tamaa na hamu zake mbaya kana kwamba tumezisulubisha kwenye msalaba."

Galatians 5:25

Kama tukiishi kwa Roho

"Tangu Roho wa Mungu alipotufanya kuwa hai"

tembea kwa Roho

Neno 'kutembea' ni sitiari kuonesha maisha ya kila siku. "mruhusu Roho Mtakatifu awaogoze ili kwamba tufanye mambo yanayompendeza na kumheshimu Mungu.

tu

"tunapaswa"

Galatians 6

Wagalatia 06 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Sura hii inahitimisha barua ya Paulo. Maneno yake ya mwisho yanashughulikia masuala ambayo hayaonekani kuwa yameunganishwa na barua yake yote.

Ndugu

Paulo anaandika maneno katika sura hii kwa Wakristo. Anawaita "ndugu." Hii inahusu ndugu za Paulo wa Kikristo na sio ndugu zake wa Kiyahudi.

Dhana maalum katika sura hii

Uumbaji Mpya

Watu ambao wamezaliwa tena ni uumbaji mpya katika Kristo. Wakristo wamepewa uzima mpya katika Kristo. Wana asili mpya ndani yao baada ya kuwa na imani katika Kristo. Kwa Paulo, hii ni muhimu zaidi kuliko ukoo cha mtu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#bornagain and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Mwili

Hili ni suala ngumu. "Mwili" inatofautishwa na "roho." Katika sura hii, mwili pia hutumiwa kutaja mwili halisi. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#flesh and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#spirit)

__<< | __

Galatians 6:1

sentensi Unganishi

Paulo alifundisha waamini jinsi wanavyopaswa kuwatendea waamini na jinsi Mungu anavyowapa thawabu.

Ndugu

Lina maana ya jamaa ya Wakristo ikijumuisha kwa pamoja wanaume na wanawake, kwa kuwa waamini wote ndani ya Kristo ni wana familia moja ya kiroho na Mungu akiwa Baba yao wa mbinguni.

Ikiwa mtu

"ikiwa mtu mmoja" au "mtu mmoja wapo miongoni mwenu"

amekamatwa katika makosa/dhambi

Maana zinazokubalika hapa ni 1) mtu amepatikana katika tendo, " amekamatwa katika kitendo cha dhambi," au 2) mtu amefanya dhambi bila kudhamiria kufanya uovu," ''amefanya dhambi."

ninyi mlio wa kiroho

"wale wanaoongozwa na Roho" au " ninyi mnaoishi chini ya uongozi wa Roho"

mrejeshe huyo mtu

"msahihishe huyo mtu aliyefanya dhambi" au "mtie moyo aliyefanya dhambi aweze kurudia mahusiano sahihi na Mungu."

katika roho ya upole

Maana zinazokubalika 1) Roho anamwelekeza mtu mwenye kutoa masahihisho au 2)" kwa mtazamo wa upole" au kwa njia ya upole" au "kwa hali ya uzuri".

Huku ukijiangalia mwenyewe

maneno haya yanahusu Wagalatia kana kwamba ni mtu mmoja, lengo ni kutilia mkazo kwamba anaongea na mtu mmoja binafsi. "Jiangalie binafsi" au "ninamwambia kila mmoja wenu" "Jiangalie mwenyewe"

ili msijaribiwe

Maneno haya yaweza kuelezwa kwa muundo tendaji. ''ili kwamba kisiwepo kitu cha kuwajaribu ninyi kutenda dhambi"

Galatians 6:3

ikiwa

"Kwa sababu." Hii neno inaonyesha kwamba maneno anayosema baadaye yatoa sababu za kwa nini Wagalatia lazima 1) "kuchukuliana mizigo" 6:1 au 2)kuwa waangalifu ili na wao wenyewe wasije wakajaribiwa (6:1) au " wasije wakajivuna (5:1)

yeye ni kitu

yeye ni mtu muhimu 'au' yeye ni bora kuliko ya wengine

Yeye si kitu

Yeye si muhimu 'au' hana bora kuliko ya wengine

Kila mmoja anapaswa

"Kila mtu lazima"

kila mmoja ataubeba mzigo wake mwenyewe

Kila mtu atahukumiwa kwa kazi yake mwenyewe tu' au 'kila mtu atawajibika kwa kazi yake mwenyewe tu"

kila mmoja ata..

"Kila mtu ata..."

Galatians 6:6

Mmoja wapo

"Mtu"

neno

Hapa hii ina maana kila kitu ambacho Mungu amesema au ameamuru, kama "neno la Mungu" au "ujumbe wa kweli."

Kila apandacho mtu, ndicho atakachovuna pia

kupanda kunamaanisha kufanya jambo fulani ambalo matokeo yake yanafanana na kitendo chenyewe. kuvuna inawakilisha matokeo ya kile ambacho mtu amefanya. "kama vile mkulima avunavyo matunda ya kile kile alichokipanda. hivyo basi, kila mtu atapata matokeo ya kile anachokifanya.

Mtu ... yake

Paulo habainishi wanaume hapa. AT "mtu ... mtu huyo"

kupanda katika mwili wake

Neno 'mwili' ni lugha ya pich kuonesha asili ya dhambi ya mtu. "hupanda mbegu sawa na matakwa ya dhambi ya asili" Anafanya mambo asili yake ya dhambi anataka kufanya"

atavuna uharibifu kutokana na mwili wake

'Atapokea adhabu kwa ajili ya kile kilichofanywa na mwili wake wenye dhambi '

kupanda katika Roho

"Anafanya mambo ya Roho wa Mungu apendayo"

Atavuna uzima wa milele kutoka kwa Roho

'Kupokea uzima wa milele kama zawadi kutoka kwa Roho wa Mungu'

Galatians 6:9

Tusichoke katika kutenda mema

"Tunatakiwa kuendelea kutenda mema"

kutenda mema

kufanya mema kwa ustawi wa watu wengine

wakati wake

"kwa wakati muafaka" au " kwa wakati ambao Mungu ameuchagua"

Hivyo basi,

"kama matoke ya" au "kwasababu ya "

hasa kwa walio

"hasa kwa wale" au "mahususi kwa wale"

walio ndani ya imani

"kwa wale walio wana familia ya Mungu kupitia imani katika Yesu"

Galatians 6:11

Sentensi kiunganishi

Paulo akikaribia kufunga waraka wake, anawakumbusha jambo moja zaidi kwamba sheria haiokoi na kwamba wanatakiwa kuumbuka msalaba wa Yesu

barua kubwa

Hii inaweza kumaanisha kwamba Paulo anasisitiza 1)maelezo yanayofuata au 2) kwamba barua hii ilitoka kwake.

kwa mkono wangu

Maana zinazokubalika 1)Huenda Paulo alikuwa na msaidizi ambaye aliandika mambo mengi katika barua hii kama vile Paulo alimwambia kuandika, lakini Paulo mwenyewe aliandika sehemu hii ya mwisho ya barua au 2) Paulo aliandika barua hii yote yeye mwenyewe.

kufanya mema kwa kuwashawishi

"kuwafanya wengine wawafikirie vizuri" au kuwafany wengine wafikiri kuwa wao ni watu wazuri"

katika mwili

"kwa ushahidi wa kuonekana" au " kwa juhudi zao"

kulazimisha

"kushurutisha" au kushawishi kwa nguvu"

Wanafanya hivyo kwa sababu wasiingie kwenye mateso ya msalaba wa Kristo

"ili kwamba Wayahudi wasiwatese kwa kusema kuwa msalaba wa Kristo pekee huokoa watu"

msalaba

Msalaba hapa unawakilisha kile ambacho Kristo alifanya kwa ajili yetu alipokufa pale msalabani. "Kazi aliyoifanya juu ya msalaba" au " kifo na ufufuo wa Yesu"

wanataka

"watu wale wanaowataka nyie mtahiriwe"

ili waweze kujivunia miili yenu

"ili kwamba wajivune kwa kuwa watakuwa wamewaongeza kwa watu wale wanaoshika sheria."

Galatians 6:14

Isitokee nikajivuna isipokuwa kwa msalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo

"sitaki kujivunia kitu chochote zaidi ya msalaba"

ulimwengu umesulubiwa kwangu

Tungo hii inaweza kuelezwa katika muundo tendaji: "Ninadhani duniani tayari imekwisha kufa" au " naichukulia dunia kama ni mharifu ambaye Mungu amemuua msalabani"

kwa ulimwengu

maneno "nimesulubiwa" yanaeleweka vizuri kutoka na maneno yaliyotangulia kabla ya haya. " na nimesulubishwa katika ulimwengu"

kwa ulimwengu

Maana zinazokubalika ni) Ulimwengu unadhania kuwa mimi tayari nimeshakufa" au "dunia inanichukulia mimi kama mharifu ambaye Mungu amemuua msalabani"

Ulimwengu

maana zinazokubalika ni 1) watu wa dunia, wale ambao hawamjali Mungu au 2) mambo yale ambayo watu wasiomjua Mungu hufikiri ni ya muhimu.

kuwa si kitu

"ni muhimu" kwa Mungu

uzao mpya

maana inawezekana ni 1) muumini mpya katika Yesu Kristo au 2) maisha mapya katika muumini.

amani na rehema juu yao, na Israeli wa Mungu

maana zinazoweza kukubalika ni 1) kwamba waumini kwa ujumla ni Israeli ya Mungu au 2) "amani na rehema ziwe juu ya waamini wa Mataifa na juu ya Israeli ya Mungu " au 3) "amani na iwe juu ya wale wanaofuata kanuni , na inaweza rehema ziwe hata juu ya Israeli ya Mungu. "

Galatians 6:17

Tangu sasa

Hii inaweza kumaanisha "mwisho" au "kwa kuhitimisha barua hii"

mtu yeyote asinitaabishe

Maana zinaweza kukubalika ni 1) Paulo anawaamuru Wagalatia wasimtaabishe "Ninawaamuru kwamba : "msinitaabishe" au 2)Paulo anawaambia Wagalatia kwamba anaagiza watu wote wasimtaabishe. "Ninamwamuru kila mmoja kwamba: usinitaabishe" au 3) Paulo anaeleza matakwa yake, "sitaki mtu yeyote anitaabishe"

kunitesa mimi

Maana zinazokubalika ni 1) "kuniambia mambo haya" au 2) kunisababishia matatizo" au "kunipa kazi ngumu."

maana nimebeba chapa za Yesu mwilini mwangu

"NIna makovuya vidonda katika mwili wangu kwa sababu ya huduma yangu kwa Yesu" au "Bado nina alama ya makovu katika mwili wangu kwasababu mimi ni mali ya Yesu"

Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe na roho

"Ninaomba kwamba Bwana Yesu atakuwa mwema katika roho zenu"

ndugu

Hapa neno 'ndugu' linamaanisha Wakristo, kwa kujumuisha wanaume na wanawake wote, kwa kuwa waumini wote ndani ya Kristo ni washirika wa familia moja, na Mungu ndiye Baba yao wa mbinguni.

Utangulizi wa Waefeso

Sehemu ya 1: Utangulizi wa Ujumla

Maelezo ya Kitabu cha Waefeso

  1. Salamu na sala kwa baraka za kiroho katika Kristo (1:1-23)
  2. Dhambi na wokovu (2:1-10)
  3. Umoja pamoja na amani (2:11-22)
  4. Siri ya Kristo ndani yenu, amejulishwa (3:1-13)
  5. Maombi kwa ajili ya utajiri wa utukufu wake ili kuwafanya kuwa na nguvu (3:14-21)
  6. Umoja wa Roho, kujenga Mwili wa Kristo (4: 1-16)
  7. Maisha mapya (4:17-32)
  8. Waigaji wa Mungu (5:1-21)
  9. Wake na waume; watoto na wazazi; watumwa na mabwana (5:22-6:9)
  10. Silaha za Mungu (6:10-20)
  11. Salamu ya mwisho (6:21-24)

Nani aliandika kitabu cha Waefeso?

Paulo aliaandika Waefeso. Paulo alikuwa anatoka mji wa Tarso. Alijulikana pia kama Saulo mwanzoni. Kabla kuwa Mkristo, alikuwa Mfarisayo na kuwatesa Wakristo. Baada ya kuwa Mkristo alitembea mara kadhaa kwa ardhi ya Warumi huku akiambia watu kuhusu Yesu.

Mtume Paulo alisaidia kuanzisha kanisa la Efeso wakati moja wa safari zake. Pia akaishi na Waefeso kwa mwaka moja na nusu akiwasaidia waumini. Pengine Paulo aliandika barua hii angali kwenye jela wa Roma.

Kitabu cha Waefeso ni kuhusu nini?

Paulo aliwaandikia barua hii Wakristo wa Waefeso kuwaeleza upendo wake Mungu kwao kupitia Yesu Kristo. Alieleza baraka Mungu alikuwa anawapa kwa sababu walikuwa wameunganishwa pamoja na Kristo. Aliwaeleza waumini wote kwamba walikuwa umoja na haikujari kama mtu ni Myahudi au Wayunani.

Je, kichwa cha kitabu hiki kinapaswa kutafsiriwaje?

Watafsiri wanaweza kuchagua kuita kitabu hiki kwa kichwa chake cha asili, "Waefeso." Au wanaweza kuchagua kichwa wazi, kama "Barua ya Paulo kwa Kanisa la Efeso" au "Barua kwa Wakristo huko Efeso." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-names)

Sehemu ya 2: Dhana muhimu za Kidini na za Kitamaduni

Je, ni nini "ukweli uliofichwa" katika Kitabu cha Waefeso?

Maneno yaliyotafsiriwa katika ULB kama "ukweli uliofichwa" au "uliofichwa" hutokea mara sita. Kwa hiyo Paulo alimaanisha kitu ambacho Mungu alipaswa kuwafunulia wanadamu kwa sababu hawakuweza kukijua wenyewe. Daima ilikuwa inahusu jinsi Mungu alivyopanga kuokoa wanadamu. Wakati mwingine ilikuwa juu ya mpango wake wa kufanya amani kati yake na wanadamu. Wakati mwingine ilikuwa juu ya mpango wake wa kuunganisha Wayahudi na Wayunani kupitia Kristo. Wayunani sasa wanaweza kufaidika na ahadi za Kristo wakiwa sawa na Wayahudi.

Je, Paulo alisema nini juu ya wokovu na kuishi kwa haki?

Paulo alisema mengi juu ya wokovu na kuishi kwa haki katika barua hii na katika barua zake nyingi. Alisema kuwa Mungu amekuwa na wema na kuwaokoa Wakristo kwa sababu wanaamini Yesu. Kwa hiyo, baada ya kuwa Wakristo, wanapaswa kuishi kwa njia ya haki ili kuonyesha kuwa wana imani katika Kristo. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous)

Sehemu ya 3: Masuala muhimu ya Tafsiri

"Wewe" kutumika kwa umoja na wingi

Katika kitabu hiki, neno "Mimi" linamaanisha Paulo. Neno "nyinyi" ni karibu kila mara na linawakilisha waumini ambao wanaweza kusoma barua hii, isipokuwa: 5:14, 6:2, na 6:3. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-you)

Je, Paulo alimaanisha nini na "Upekee

Wakati Paulo alizungumza kuhusu "nafsi mpya" au "mtu mpya," alimaanisha hali mpya ambayo muumini anapokea kutoka kwa Roho Mtakatifu. Hali hii mpya iliumbwa kwa mfano wa Mungu (Angalia: 4:24). Maneno "mtu mpya" hutumiwa pia kwa ajili ya Mungu kuleta amani kati ya Wayahudi na Wayunani. Mungu aliwaunganisha kama watu mmoja ambao ni wake (Tazama: 2:15).

Paulo alimaanisha nini na "nafsi mpya" au "mtu mpya"?

Wakati Paulo alizungumza kuhusu "nafsi mpya" au "mtu mpya," alimaanisha hali mpya ambayo muumini anapokea kutoka kwa Roho Mtakatifu. Hali hii mpya iliumbwa kwa mfano wa Mungu (Angalia: 4:24). Maneno "mtu mpya" hutumiwa pia kwa ajili ya Mungu kuleta amani kati ya Wayahudi na Wayunani. Mungu aliwaunganisha kama watu mmoja ambao ni wake (Tazama: 2:15)

Je, mawazo ya "takatifu" na "takasa" yanawakilishwa vipi katika Waefeso katika ULB?

Maandiko hutumia maneno kama hayo ili kuonyesha yoyote kati ya mawazo mbalimbali. Kwa sababu hii, mara nyingi ni vigumu kwa watafsiri kuyawakilisha vizuri katika tafsiri zao. Katika kutafsiri kwa Kiingereza, ULB inatumia kanuni zifuatazo:

Wakati mwingine maana katika kifungu ina maana ya utakatifu wa maadili. Hasa muhimu kwa kuelewa injili ni matumizi ya "takatifu" kuonyesha ukweli kwamba Mungu anawaona Wakristo kama wasio na dhambi kwa sababu wameungana na Yesu Kristo. Matumizi mengine ya "takatifu" ni kueleza wazo kwamba Mungu ni mkamilifu na hana hatia. Matumizi ya tatu ni kueleza wazo kwamba Wakristo wanapaswa kuwa na mwenendo isiyo na hatia, na kasoro katika maisha yao. Katika hali hizi, ULB inatumia "takatifu," "Mungu mtakatifu," "watakatifu," au "watu watakatifu." (Angalia: 1:1, 4)

Wakati mwingine maana katika kifungu inaonyesha Wakristo bila kuashiria jukumu fulani wanalopaswa kufanya. Katika hali hizi, ULB inatumia "mwumini" au "waumini."

Wakati mwingine maana katika kifungu kinaashiria wazo la mtu au kitu kiichowekwa wakfu kwa Mungu pekee. Katika hali hizi, ULB inatumia "kutenga," "kukusudia," au "kuhifadhiwa kwa." (Angalia: 3:5)

UDB mara nyingi husaidia wakati watafsiri wanafikiri juu ya jinsi ya kuwakilisha mawazo haya katika tafsiri zao wenyewe.

Je, Paulo alimaanisha nini kwa maneno "katika Kristo," "katika Bwana," nk?

Aina hii ya usemi hutokea katika 1:1, 3, 4, 6, 7, 9, 10, 11, 12, 13, 15, 20; 2:6, 7, 10, 13, 15, 16, 18, 21, 22; 3:5, 6, 9, 11, 12, 21; 4:1, 17, 21, 32; 5:8, 18, 19; 6:1, 10, 18, 21. Paulo alimaanisha kueleza wazo la muungano wa karibu sana kati ya Kristo na waumini. Tafadhali angalia utangulizi wa Kitabu cha Warumi kwa maelezo zaidi juu ya aina hii ya usemi.

Je, ni masuala gani muhimu katika Kitabu cha Waefeso?

(See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/jit.html#translate-textvariants)

Ephesians 1

Waefeso 01 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

"Naomba"

Paulo amepanga sehemu ya sura hii kama sala ya sifa kwa Mungu. Lakini Paulo hazungumzi na Mungu pekee. Anafundisha kanisa huko Efeso. Pia anawaambia Waefeso jinsi anavyowaombea.

Dhana maalum katika sura hii

Kujaaliwa

Wasomi wengi wanaamini kwamba sura hii inafundisha juu ya somo inayojulikana kama "kujaaliwa." Hii inahusiana na dhana ya Biblia ya "kujaaliwa." Wasomi wengine huchukua hii kuonyesha kwamba Mungu amechagua, tangu kabla ya msingi wa dunia, baadhi ya watu ili kuwaokoa milele. Wakristo wana maoni tofauti juu ya kile Biblia inafundisha juu ya suala hili. Kwa hivyo watafsiri wanahitaji kuwa makini zaidi wakati wa kutafsiri sura hii, hasa kuhusiana na mambo ya usababisho. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#predestine)

| >>

Ephesians 1:1

Sentensi Unganishi

Majina ya Paulo peke yake kama mwandishi wa hii barua kwa waamini wa kanisa la Efeso

Maelezo ya Jumla

Bila kutajwa vinginevyo, pote palipo na " kwenu" na "Yako" ya husu waamini wa Efeso pamoja na waamini wote na kwa hiyo ni wingi.

Paulo, Mtume ... Kwa watakatifu wa Mungu Efeso

Lugha yako yaweza kuwa na namna ya kumtambulisha mwandishi wa barua na waliokusudiwa. " Mimi, Paulo, Mtume na waandikia hii barua kwenu, watu watakatifu wa Mungu Efeso.

Walio waaminifu katika Kristo

"Katika Kristo Yesu" na misemo kama hiyo ni mifano inayo jitokeza kwenye barua za agano jipya. Zinaeleza mahusiano madhubuti sana kati ya Kristo na ao wanao mwamini.

Neema kwenu na amani.

Hii ni salamu zoefu na baraka ambayo Paulo utumia kwenye barua zake.

Ephesians 1:3

Sentensi unganishi

Paulo anafungua barua kwa kuongea kuhusu nafasi ya waamini na usalama wao mbele za Mungu.

Maelezo ya Jumla

Katika hiki kitabu, vinginevyo kuelezwa, maneno "sisi" na "wote" ya husu Paulo, waamini wa Efeso, na waamini wote.

Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo apewe sifa.

'Hii pia yaweza ekwa hali tendaji. " Acha tumsifu Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo.

Aliyetubariki

"kwa kuwa Mungu ameyubariki sisi"

Kila baraka za rohoni

"Kila baraka zinakuja kutoka katika Roho wa Mungu"

Katika maeneo ya bingu

"katika ulimwengu wa roho". Neno "bingu" la husu mahali Mungu alipo.

Ndani ya Yesu

"Ndani ya Yesu " sawa na maelezo ambayo ni mafumbo kila mara hutokea kwenye barua za Agano jipya. Zinaeleza aina ya mahusiano mazito yanayowezekana kati Kristo na wote wanaomwamini.

Tuwe watakatifu na tusiwe na lawama

Paulo anatumia maneno mawili yenye kufanana akisisitiza uadilifu.

Ephesians 1:5

Maelezo ya Jumla

Maneno "wake", "Yeye", na "yeye" yamuhusu Mungu.

Mungu ametutangazia sisi kuwa warithi wake

Neno' sisi' linamhusu Paulo, Kanisa la Efeso, na waamini wote ndani ya Kristo."Mungu alipanga muda mrefu kuturithi."

Kuwa urithi

Hapa " warithi" inahusu kuwekwa ndani ya familia ya Mungu.

Kupitia Yesu Kristo

Mungu aliwaleta waamini kwenye familia yake kupitia kazi ya Yesu Kristo.

Mpendwa wake wa kipekee

"Mpendwa wake pekee, Yesu Kristo" au "Mwanae, anaye mpenda"

Ephesians 1:7

Kwa mwana wake wa kipekee

"kwa mwana wa Mungu wa kipekee, Yesu Kristo"

Utajiri wa neema yake

Paulo anazungumzia neema ya Mungu kana kwamba ilikuwa ni vitu vya thamani: "ukuu wa neema ya Mungu" au "kushikamana na neema ya Mungu"

Ametumwagia hii neema kwa sana

"Ametupa sisi hiki kiasi kikubwa cha neema" au " Amekuwa mkarimu sana kwetu"

katika hekima na ufahamu

Yamkini tafsiri zilizopo ni 1) "sababu anayo hekima zote na ufahamu" 2) "ilituwe na hekima kubwa na ufahamu"

Ephesians 1:9

kwa kadiri ya alivyo pendezwa

Yamkini tafsiri zilizopo ni 1) "sababu alitaka kutufahamisha" au 2) " ndivyo alivyo taka"

na aliyo ionyesha katika Kristo

"na alionyesha kusudi hili ndani ya Kristo

katika Kristo

"kwa njia ya Kristo"

kwa lengo la kuwa na mpango

Sentensi mpya ya weza anza hapa. " Alifanya hivi kwa lengo la kuwa na mpango" au "Alifanya hivi, akifikiria kuhusu mpango.

kwa wakati timilifu

"Kwa kuwa wakati ukiwa mwafaka" au "kwa wakati aliyo uteuwa"

Ephesians 1:11

Tulichaguliwa kuwa warithi

Hii yaweza nenwa kama kauli tendaji. "Mungu ametuchagua sisi kuwa warithi"

Tumechaguliwa... ni sisi ambao ni wa kwanza

"Mungu alituchagua hapo awali"

Ili kwamba tuwe wa kwanza

Hapa neno "sisi" la husu wa Yahudi waamini walio sikia habari njema, sio waamini wa Efeso.

Ili kwamba tuwe sifa za utukufu wake

"ili kwamba tuishi kumsifu kwa utukufu wake.

Ephesians 1:13

Tumetiwa mhuri na ahadi ya Roho Mtakatifu

Nta ilikuwa ya wekwa kwenye barua na kuchapwa na alama inayowakilisha nani katuma barua. Paulo anatumia huu utamaduni kutuonyesha picha jinsi gani Mungu amemtumia Roho Mtakatifu kutu hakikishia kwa sisi ni wake. "Mungu aliweka mhuri wokovu wetu na Roho Mtakatifu akionyesha umiliki wake."

Dhamana ya urithi wetu

Kupokea ahadi ya Mungu ya zungumziwa hapa kama vile mtu anavyo rithi mali au utajiri kutoka katika familia. "ahadi ya kuwa tutapokea kile ambacho Mungu ametuahidi"

Ephesians 1:15

Sentensi unganishi

Paulo anaomba kwa ajili ya waamini wa Efeso na anamsifu Mungu kwa ajili ya nguvu waliyo nayo kupitia Kristo.

Sijaacha kumsifu Mungu

Paulo anatumia "sijaacha" kusisitiza kuwa anaendelea kumsifu Mungu. "Naendelea kumshukuru Mungu"

Ephesians 1:17

roho ya hekima na mafunuo ya ufahamu wake

":hekima ya kiroho ya kufahamu mafunuo yake"

macho yenu ya moyoni yatiwe nuru

"kipengele macho ya rohoni "inaelezea uwezo wa mtu kupata ufahamu.'kwamba upate ufahamu na kutiwa nuru."

macho yenu ya moyoni yatiwe nuru

Hii yawezwa tajwa kama njeo tendaji. Ili Mungu awatie nuru mioyo yenu" au "kwamba Mungu awatie nuru ufahamu wenu"

kutiwa nuru

"kufanywa kuona"

urithi

Kupokea kile ambacho Mungu amewaahidi waamini, ya elezewa kana kwamba mtu anarithi mali na utajiri kutoka kwa nduguye wa familia.

watakatifu wote wa Mungu

Hii yawezwa tajwa kama njeo tendaji. "Wote wale ambao amewatenga kwa ajili yake" au "wote wale ambao ni wake kabisa"

Ephesians 1:19

ukuu uzidio wa nguvu yake

Nguve za Mungu za pita sana nguvu zingine.

ndani yetu

"kwa faida yetu" au "kwa uhusiano nasi"

kufanya kazi katika nguvu zake

"nguvu yake kubwa ambayo ya fanya kazi ndani yetu"

alimfufua kutoka kwa wafu

"alimfufua kutoka kwa wafu" au "alimfanya kuishi tena"

kumketisha katika mkono wake wa kuume

"Kristo aliye keti mkono wa kuume wa Mungu" au "kristo aliye keti sehemu ya adhama"

mahali pa mbingu

"katika ulimwengu wa roho". Neno "mbingu" la husu sehemu Mungu alipo. Ona jinsi illivyo tafsiriwa katika 1:3

juu mbali na utawala, mamlaka, nguvu, enzi

Hii ni misemo tofauti ya matabaka ya viumbe wa rohoni, kwa malaika na mapepo. " mbali zaidi ya aina tofauti za viumbe wa rohoni"

kila jina litajwalo

Hii ya weza tajwa katika kauli tendaji. Tafsiri zilizopo ni 1) "Kila jina mwanadamu atoalo" au 2) "Kila jina Mungu atoalo"

Jina

Tafsiri zilizopo ni 1) Cheo au 2)nafasi ya mamlaka.

wakati huu

"Katika wakati huu"

wakati ujao

"hapo baadae"

Ephesians 1:22

Mungu amevitiisha

Mungu ameweka" au "Mungu ameweka"

vitu vyote chini ya miguu ya Kristo

Hapa miguu inawakisha ubwana wa Kristo,mamlaka,na nguvu:"vitu vyote chini ya nguvu ya Kristo"

alifanya yeye kichwa ...ambacho ni mwili wake

kama mwili wake ,kichwa hutawala vitu vyote vinavyohusu mwili wake hivyo ni Kristo kichwa cha mwili wa kanisa.

Kichwa cha vitu vyote katika kanisa

Hapa "kichwa" kinahusu kiongozi au mmoja ambaye yupo kwenye madaraka "mtawala juu ya vitu vyote ndani ya kanisa."

ambacho ni mwili wake

Kanisa kila mara hurejea mwili wa Kristo.

"ukamilifu wake ambao hujaza vitu vyote katika njia zote"

"Kristo hujaza kanisa na kwa mwili wake na nguvu ambazo hutupatia na kuzuilia maisha na vitu vyote"

Ephesians 2

Waefeso 02 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Sura hii inazingatia maisha ya Mkristo kabla ya kumwamini Yesu. Kwa hiyo Paulo anatumia habari hii kuelezea namna maisha ya zamani ya mtu ilivyo tofauti na utambulisho mpya wa Mkristo "katika Kristo." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith)

Dhana maalum katika sura hii

Mwili mmoja

Paulo anafundisha kuhusu kanisa katika sura hii. Kanisa lina makundi mawili tofauti ya watu (Wayahudi na Wayunani). Wao sasa ni kundi au "mwili" mmoja. Kanisa linajulikana pia kama mwili wa Kristo. Wayahudi na Wayunani wameunganishwa katika Kristo.

Mifano muhimu ya matamshi katika sura hii

Wamekufa katika makosa na dhambi"

Paulo anafundisha kwamba wale ambao si Wakristo "wamekufa" katika dhambi zao. Dhambi huwafunga au huwafanya kuwa watumwa. Hii inawafanya kuwa "wamekufa" kiroho . Paulo anaandika kwamba Mungu huwafanya Wakristo kuwa hai katika Kristo. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#death, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

Maelezo ya kuishi kidunia

Paulo anatumia njia nyingi za kuelezea jinsi ilivyo dunia ya wasio Wakristo. "Waliishi kulingana na njia za ulimwengu huu" na "wanaishi kulingana na kiongozi wa mamlaka ya hewa," "kutimiza matamanio mabaya ya asili yetu ya dhambi," na "kutekeleza matamanio ya mwili na ya akili. "

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"(hilo) Ni zawadi ya Mungu"

Wasomi fulani wanaamini "hilo" hapa linamaanisha kuokolewa. Wasomi wengine wanaamini kwamba ni imani ambayo ni zawadi ya Mungu. Kwa sababu ya maandishi ya Kigiriki, "hilo" inamaanisha kuokolewa na neema ya Mungu kupitia imani.

Mwili

Hii ni suala ngumu. "Mwili" ina uwezekano wa kuwa mfano wa asili ya dhambi ya mtu. Maneno ya "Wayunani kimwili" yanaonyesha Waefeso wakati mmoja waliishi bila ya kumjali Mungu. "Mwili" pia hutumiwa katika aya hii kutaja sehemu ya kimwili ya mwanadamu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#fles)

<< | >>

Ephesians 2:1

Sentensi Unganishi:

Paulo anawakumbusha waamini walivyokuwa hapa mwanzo na sasa namna walivyo mbele za Mungu.

Na ninyi mlikuwa wafu katika makosa na dhambi zenu

Hii inaonyesha ni kwa namna gani watu wana dhambi kiasi cha kushindwa kumtii Mungu kwa namna ile ile wafu wasivyoweza kujishughulisha kimwili tena.

makosa na dhambi zenu

Maneno "makosa" na "dhambi" kimsingi yanamaanisha kitu kile kile. Paulo anayatumia yote pamoja kuweka mkazo wa ukubwa wa dhambi ya watu.

hapo mwanzo mlienenda

Hii inaelezea tabia ya namna watu walivyoishi

kwa kumfuata mtawala wa mamlaka ya anga

Mtume Paulo anatumia neno "anga" kumaanisha tabia za ubinafsi na ufisadi wa watu waaishio humu duniani.

mtawala wa mamlaka ya anga

Hii inamaanisha ibilisi au shetani

roho yake yule

Sentensi "roho yake yule" inamaanisha ibilisi au shetani.

Tulikuwa tukitenda kwa namna ya tamaa mbaya za miili yetu, tulikuwa tukifanya mapenzi mwili na ya akili.

Maneno "mwili" na "nia" yanawakilisha mwili wote.

wana wa ghadhabu

Watu ambao Mungu amewakasirikia

Ephesians 2:4

Mungu ni mwingi wa rehema

"Mungu amejaa rehema" au "Mungu ni mwema sana kwetu"

kwa sababu ya pendo lake kubwa alilotupenda sisi

"kwa sababu ya pendo lake kubwa kwetu" au "kwa sababu anatupenda sana"

wakati tulipokuwa wafu katika makosa yetu, alituleta pamoja katika maisha mapya

Hii inaonyesha ni jinsi gani mtu mwenye dhambi hawezi kumtii Mungu mpaka pale anapopewa maisha mapya ya kiroho kama tu vile mtu mfu asivyoweza kujishughulisha na maisha ya mwili huu isipokuwa amefufuliwa kutoka katika wafu.

alituleta pamoja katika maisha mapya ndani ya Kristo

"Ndani ya Kristo" na maelezo kama hayo ni mifano ambayo mara nyingi hutokea katika barua au nyaraka za Agano Jipya. Inaelezea aina nzito kabisa ya mahusiano inayoweze kuwepo kati ya Kristo na wote wanaomwamini.

alitufufua pamoja na kutufanya kukaa pamoja katika ulimwengu wa roho ndani ya Kristo Yesu.

Kama alivyokwisha kumfufua Kristo, atatufufua na sisi na tutakuwa na Kristo mbinguni.

ndani ya Kristo Yesu

"Ndani ya Kristo" na maelezo kama hayo ni mifano ambayo mara nyingi hutokea katika barua au nyaraka za Agano Jipya. Inaelezea aina nzito kabisa ya mahusiano inayoweza kuwepo kati ya Kristo na wote wanaomwamini.

katika nyakati zijazo

"huko baadaye"

Ephesians 2:8

Kwa maana ni kwa neema mmeokolewa kwa njia ya imani

Wema wake Mungu kwetu ni sababu iliyotuwezesha sisi kuokolewa kutoka katika hukumu kama tu tutamwamini Yesu.

Haitokani na

Neno "haitokani" linahusu au linarejea kwamba "kwa neema mmeokolewa kwa njia ya imani"

...kutoka kwetu

Neno "kwetu" linaelezewa kumaanisha Paulo na waamini wote katika Efeso.

sisi tu kazi ya Mungu

Neno "sisi" linaelezewa kumaanisha Paulo na waamini wote katika Efeso

katika Yesu Kristo

"Ndani ya Kristo" na maelezo kama hayo ni mifano ambayo mara nyingi hutokea katika barua au nyaraka za Agano Jipya. Inaelezea aina nzito kabisa ya mahusiano inayoweza kuwepo kati ya Kristo na wote wanaomwamini.

Ephesians 2:11

Maelezo au Sentensi unganishi:

Paulo anawakumbusha hawa waamini kwamba Mungu aliwafanya watu wamataifa na Wayahudi kuwa mwili mmoja kupitia Kristo na msalaba wake.

wamataifa kwa jinsi ya mwili

Hii inaongelea juu watu ambao hawakuzaliwa Wayahudi.

msiyotairiwa

Watu ambao si Wayahudi hawakutairiwa walipokuwa watoto na hivyo Wayahudi waliwaona hao kama watu wasiomfuata Mungu.

tohara

Hili lilikuwa neno lingine linaloelezea juu ya Wayahudi kwa sababu watoto wote wachanga wa kiume walitairiwa walipokuwa na umri wa siku nane.

tohara ya mwili

Kutahiriwa kulifanywa juu ya miili ya watoto wadogo wa kiume.

watu wa Israel

"jamii ya watu wa Israel"

wageni kwa agano la ahadi

Tafsiri mbadala: "hamkujua ahadi za agano la Mungu"

Ephesians 2:13

Sasa katika Kristo Yesu

Paulo anawatofautisha Waefeso kabla ya kumwamini Kirsto na baada ya kumwamini Kristo

ninyi ambao hapo mwanzo mlikuwa mbali na Mungu, mmeletwa karibu na Mungu

Kwa sababu ya dhambi za waamini, walikuwa wametengwa na Mungu. Hata hivyo, sasa Yesu amewaleta karibu na Mungu kwa damu yake.

yeye ndiye amani yetu

Tafsiri mbadala: "Yesu hutupa amani yake"

Kwa mwili wake

Tafsiri mbadala: "Kwa kifo chake juu ya msalaba"

ukuta wa utenganisho

Tafsiri mbadala: "ukuta wa chuki" au "nia mbaya"

umetutenganisha

Herufi za kwanza "ume" zinaelezea kwamba huo ukuta uliwatenganisha wote Paulo na Waefeso, ambao uliwatenga waumini wa Kiyahudi kutoka kwa waumini wasiokuwa Wakiyahudi (wamataifa)

aliiondoa sheria ya amri na kanuni

Damu ya Yesu ilileta utoshelevu wa sheria ya Musa ili kwamba wote Wayahudi na watu wa mataifa wanaweza kuishi kwa amani ndani ya Mungu.

mtu mmoja mpya

Mtu mmoja mpya, mtu wa jamii ya watu waliokombolewa.

ndani yake

Ni muunganiko na Yesu ambao unafanya upatanisho uwezekane kati ya Wayahudi na watu wa mataifa.

kuwapatanisha watu wote

Tafsiri mbadala: "kuwaleta pamoja wote wawili yaani Wayahudi na watu wa Mataifa (wamataifa)"

kupitia msalaba...kwa njia ya msalaba

Hii ni kwamba, kwa njia ya Kifo cha Kristo juu ya msalaba.

aliufisha (aliuua) uadui kwa msalaba

Yesu aliondoa kabisa sababu ambayo iliwafanya Wayahudi na watu wa mataifa kuwa maadui. Hawakuhitajika tena kuishi kulingana na sheria ya Musa.

Ephesians 2:17

Maelezo au Sentensi Unganishi.

Paulo anawaambia waamini wakiefeso kwamba watu wa mataifa walioamini wamefanyika wamoja na mitume na manabii, na ni hekalu kwa Mungu katika Roho Mtakatifu.

amani iliyotangazwa

Tasfiri mbadala: "injili ya amani iliyotangazwa" au "injili ya amani iliyotangazwa kwa uwazi"

ninyi mliokuwa mbali

Hii inazungumzia juu ya watu wa mataifa au wale wasio Wayahudi.

wale waliokuwa karibu

Hii inazungumzia juu ya Wayahudi.

Kwa maana kwa njia ya Yesu sisi sote wawili tuna nafasi.

Hapa "sisi sote wawili" inazungumzia juu ya Paulo, waamini wa Kiyahudi na waamini wasio Wayahudi.

kwa yule Roho Mtakatifu

Waamini wote, yaani Wayahudi na watu wa mataifa, wamepewa haki ya kuingia mbele za uwepo wa Mungu Baba kwa Roho Mtakatifu yule yule.

Ephesians 2:19

ninyi watu wa mataifa si wageni na wasafiri tena. bali ni wenyeji pamoja na wale waliotengwa kwa ajili ya Mungu na wajumbe wa nyumbani mwa Mungu.

Hii inaelezea hali ya kiroho ya watu wa mataifa kabla na baada ya kuwa waamini kwa namna ile ile ambayo watu wasiokuwa raia wanavyoweza kuwa raia wa taifa fulani.

si wageni tena

" si watu wa nje tena"

na wasafiri

"na watu wasio raia"

mmejengwa juu ya msingi

Paulo analinganisha Familia ya Mungu na jengo. Yesu akiwa jiwe kuu la pembeni, na mitume wakiwa ndiyo msingi na waamini wakiwa boma (jengo lenyewe)

jengo lote limeungamanishwa pamoja na kukuwa kama hekalu.

Paulo anaendelea kulinganisha Familia ya Kristo na jengo. Kwa namna ile ile ambayo mjenzi anaungamanisha mawe pamoja wakati akijenga, vivyo hivyo Kristo anatuungamanisha pamoja.

ndani yake...ndani ya Bwana

Haya ni maelezo ya mfano juu ya "ndani ya Kristo Yesu". Haya yanatokea mara nyingi katika nyaraka (barua) za Agano Jipya. Yanaelezea uhusiano wa nguvu sana unaoweza kuwepo baina ya Kristo na wale wanaomwamini yeye.

ninyi nanyi mnajengwa pamoja kama mahali pa kuishi pa Mungu katika Roho

Hii inaeleza namna waamini wanawekwa pamoja kuwa mahali ambapo Mungu ataishi siku zote kupitia nguvu ya Roho Mtakatifu

Ephesians 3

Waefeso 03 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

"Naomba"

Paulo amepanga sehemu ya sura hii kama sala kwa Mungu. Lakini Paulo hazunguzi na Mungu pekee. Anaombea na kufundisha kanisa huko Efeso.

Dhana maalum katika sura hii

Siri

Paulo anaashiria kanisa kama "siri". Jukumu la kanisa katika mipango ya Mungu wakati mmoja halikujulikana. Lakini Mungu amelifunua sasa. Sehemu ya siri hii inahusisha Wayunani kuwa sawa na Wayahudi katika mipango ya Mungu.

<< | >>

Ephesians 3:1

kauli unganishi

Kufanya wazi ukweli siri kuhusu kanisa kwa waumini, Paulo anataja nyuma umoja wa Wayahudi na Mataifa na hekalu la ambayo waumini sasa ni sehemu.

Kwasababu ya hii

"Kwasababu ya neema ya Mungu kwako"

mfungwa wa Kristo Yesu

"moja ambaye Kristo Yesu amemuweka katika gereza"

usimamizi wa zawadi ya Mungu kwamba yeye alinipa kwa ajili yenu

"Wajibu Mungu alinipa kusimamia neema yake juu yenu"

Ephesians 3:3

kutokana na jinsi ufunuo ulivyo funuliwa kwangu

Hii inaweza alisema katika fomu ya kazi. AT: "nini Mungu alinifunulia"

nililivyoyokuandikia kwa kifupi kwenye barua nyingine.

Paulo anataja barua nyingine ameandika kwa watu hawa.

Kwa vizazi vingine ukweli huu haukufanywa utambulike kwa watoto wao

"Ambayo Mungu hakufanya anajulikana kwa watu katika siku za nyuma"

Ila kwa sasa umewekwa wazi kwa Roho

"Sasa Roho umebaini" au "sasa Roho imefanya ni maalumu"

mitume wake na manabii wenye kuwekwa wakfu

"mitume na manabii ambao Mungu amewatenga kwa utumishi"

Ephesians 3:6

Watu wa mataifa ni warithi wenzake ... kwa njia ya Injili

Huu ni ukweli ulio fichika Paulo anaanza kuelezea katika mstari uliopita. Watu wa mataifa waliompokea Kristo pia watapokea urithi kama kama waumini wa Kiyahudi.

wanachama wenzake wa mwili

Kanisa ni mara nyingi hujulikana kama mwili wa Kristo.

katika Kristo Yesu

"Katika Kristo Yesu" na maneno kama ni mafumbo ambayo mara nyingi yametokea katika Agano Jipya. Yanaelezeamahusiano ya nguvu inawezekana kati ya Kristo na walio amini katika Yeye.

Kupitia Injili

Maana inawezekana ni 1) kwa sababu ya Injili watu wa mataifa ni washiriki wengine wa ahadi au 2) kwa sababu ya Injili watu wa mataifa ni warithi na viungo vya mwili na washirika wenzake katika ahadi.

Ephesians 3:8

Mungu amenipa zawadi hii japo kuwa mimi ni mtu mdogo kati ya wale wanaopata nafasi kwa Mungu

"Ingawa mimi ni mdogo anastahili watu wote wa Mungu, Mungu amenipa zawadi hii ya neema"

kuleta kila mtu katika mwanga na kuwaambia kuhusu mpango wa siri za Mungu

"kuwafanya watu wote kufahamu mpango wa Mungu"

kuwaambia kuhusu mpango wa siri wa Mungu kwamba Mungu (aliyeviumba vitu vyote) alikuwa amejificha kwa miaka katika siku za nyuma

"kitu ambacho Mungu alikificha kwa mda mrefu uliopita. Alipo umba kila kitu"

wale waliotengwa kwa Mungu

Hii inaweza semwa katika: "wale ambao Mungu amewatenga kwa ajili yake mwenyewe "

usiopimika

haiwezekani kujulikana kabisa

utajiri wa Kristo

Paulo anazungumzia ukweli kuhusu Kristo na baraka yeye huleta kana kwamba vilikuwa utajiri wa mali.

kuwaelimisha watu wote kuhusu mpango wa siri wa Mungu ni nini.

"angaza mwanga kwenye mpango wa Mungu ili watu wote wajue ni nini" au "kuwaambia watu wote ni nini mpango wa siri ya Mungu"

uliofichwa kwa miaka mingi kuanzia mwanzo Mungu alivyoumba kila kitu.

Hii inaweza semwa kama: "Kwamba Mungu, aliyeviumba vitu vyote, alikuwa ameficha kwa umri mrefu katika siku za nyuma"

Ephesians 3:10

viongozi na mamlaka yaliyopo mbinguni zitakuja kujulikana pande nyingi za asili ya hekima ya Mungu

ilikuwa upande asili ya hekima ya Mungu - "Mungu atafanya hekima yake kubwa ijulikane kwa viongozi na mamlaka katika ulimwengu wa roho kupitia Kanisa "

pande nyingi za asili ya hekima ya Mungu

ilikuwa upande asili ya hekima ya Mungu - hekima ya Mungu tata

watawala na mamlaka

Maneno haya yanashiriki maana sawa. Paulo anatumia yote pamoja na kusisitiza kwamba kila kiumbe cha kiroho watajua hekima ya Mungu.

kulingana na mpango wa milele

"katika kutunza mpango wa milele" au "sambamba na mpango wa milele"

katika Kristo Yesu Bwana wetu

Kwa njia ya Kristo

katika ulimwengu wa roho

Kuona jinsi ya kutafsiriwa hii angalia 1:3

Ephesians 3:12

kauli unganishi

Paul anamsifu Mungu katika mateso yake na anaomba kwa ajili ya waumini hawa wa Efeso.

upatikanaji kwa kujiamini

"upatikanaji katika uwepo wa Mungu kwa kujiamini" au "uhuru wa kuingia katika uwepo wa Mungu kwa ujasiri"

kwa sababu ya imani yetu kwake

"kwa sababu ya imani yetu katika Kristo"

tuna ujasiri

"sisi bila hofu" au "tuna ujasiri"

kujiamini

"hakika" au "uhakika"

Huu ni utukufu wako

Hapa "utukufu wako" kujisikia katika ufalme ujao. Wakristo wa Efeso wanapaswa kujivunia mateso ya Paulo gerezani. "Hii ni kwa manufaa yako" au "unapaswa ujivunie hii"

Ephesians 3:14

Kwa sababu hiyo

"Kwa sababu Mungu amefanya yote haya kwa ajili yenu"

Napiga magoti kwa Baba

"Nina inama chini kwa maombi kwa Baba" au "Mimi kwa unyenyekevu kumwomba Baba"

kwa kupitia kwake kila familia hapa duniani na minguni imetajwa

kitendo cha kumtaja hapa pengine pia inawakilisha kitendo cha kujenga: "aliyeumba na kutaja jina kila familia mbinguni na duniani"

Namwomba Mungu wewe

"kuwa angeweza kukupa"

kwamba akubariki, kutokana na utajiri wa baraka zake, akufanye imara kwa nguvu

"Mungu, kwa sababu yeye ni kubwa sana na myenye nguvu, anaweza kuruhusu wewe kuwa na nguvu kwa uwezo wake"

Awajalieni

"angetoa"

Ephesians 3:17

kauli unganishi

Paulo anaendelea maombi aliyoyaanza

kwamba Kristo aishi ndani ya mioyo yenu kupitia imani. Ninaomba kwamba muwe na shina na msingi wa upendo wake

Hili ni ombi la pili Paulo anaomba kwamba Mungu "awapatie" Waefeso "kulingana na utajiri wa utukufu wake "; kwanza ni kwamba wangeweza "kuimarishwa"

mioyo kwa njia ya imani

hapa "moyo" inawakilisha utu wa ndani, na "kupitia" inaonyesha njia ambayo Kristo anaishi ndani ya muumini. Kristo anaishi katika mioyo ya waumini kwa sababu neema ya Mungu inaruhusu wao kuwa na imani.

imani. Ninaomba kwamba muwe na shina na msingi wa upendo wake. Uwe katika pendo lake ili uweze kuelewa

maana inawezekana ni 1) "Imani. Naomba kwamba utakuwa na mzizi na msingi katika upendo wake ili uweze kuelewa" au 2) "Imani hivyo utakuwa na mzizi na msingi katika upendo wake. Nina omba pia uweze kuelewa "

kwamba muwe na shina na msingi wa upendo wake

Paulo analinganisha imani yao kwa mti wenye mizizi au nyumba iliyojengwa juu ya msingi imara. "kwamba utakuwa kama mti wenye shina zuri na nyumba yenye msingi wa jiwe."

Ili uweze kuelewa

Hili ni ombi la pili ambalo Paulo anapiga magoti yake na kuomba: la kwanza ni, Mungu awape kuimarishwa na kwamba Kristo aishi ndani ya mioyo yao kupitia Imani. na "uelewa" ni kitu cha kwanza kabisa Paulo aliomba kwamba Wafilipi wenyewe waweze kufanya.

waaminio wote

"waaminio ndani ya Kristo" au "watakatifu woote"

upana, urefu, kimo, na kina cha upendo wa Kristo

Paulo anatumia maneno hayo kuelezea kwa namba gani ambayo Kristo anatupenda.

ili upate kujua ukuu wa upendo wa Kristo

Hili ni jambo la pili kwamba Paulo anaomba kwamba Waefeso wataweza kufanya; kwanza ni kwamba wao "waelewa." "kwamba uweze kujua ukuu wa upendo wa Kristo"

ili mpate kujazwa na ukamilifu wote wa Mungu

Hili ni ombi la tatu ambalo Paulo anapiga magoti yake na kuomba: la kwanza ni,mpate "kuimarishwa" na la pili ni kwamba "muweze kuelewa"

Ephesians 3:20

kauli unganishi

Paulo anamalizia sala yake kwa baraka.

Maelezo ya ujumla:

maneno "sisi" na "sisi" katika kitabu hiki yanaendelea kuwahusisha Paul na waaminio wote.

Sasa kwake

"Sasa kwa Mungu, ambaye"

kila kitu mbali, mbali juu

Mungu anaweza kufanya zaidi kuliko tunayoweza milele kuomba au kufikiria.

Ephesians 4

Waefeso 04 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri huweka kila mstari wa mashairi kuwa upande wa kulia zaidi kuliko maandiko yote ili iwe rahisi kusoma. ULB inafanya hii kwa mstari wa 8, ambayo imenukuliwa kutoka Agano la Kale.

Dhana maalum katika sura hii

Vipawa vya kiroho

Vipawa vya kiroho ni uwezo usio wa kawaida ambao Roho Mtakatifu huwapa Wakristo baada ya kumwamini Yesu. Paulo anataja hapa baadhi tu ya vipawa vya kiroho. Wasomi wengine wanaamini kwamba Roho Mtakatifu alitoa vipawa vya kiroho kwa waumini katika kanisa la kwanza pekee. Vipawa hivi vya kiroho vilikuwa msingi kwa kuendeleza kanisa. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith)

Umoja

Paulo anaona kuwa ni muhimu sana kwamba kanisa lina umoja. Hii ni mada kuu ya sura hii.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Mtu wa kale na mtu mpya

Neno "mtu wa kale" labda linamaanisha hali ya dhambi ambayo mtu huzaliwa. "Mtu mpya" ni asili mpya au maisha mapya ambayo Mungu humpa mtu baada ya kumwamini Kristo.

<< | >>

Ephesians 4:1

kauli unganishi

Kwasababu ya kile Paulo amekuwa akiwaandikia Waefeso, anawatia moyo namna gani kuishi maisha yao kama waamini na tena anasisitiza umoja wa waamini.

Kama mfungwa kwa ajili ya Bwana

"kama mtu ambaye yuko gerezani kwa sababu ya uchaguzi wake wa kumtumikia Bwana"

Nawasihi ninyi kuishi maisha yanayoendana na wito

Neno "ninyi" linamaanisha Waefeso waamini. AT: "Nawatia moyo ninyi kujitunza wenyewe kwa namna nzuri ya wito."

Kwa unyenyekevu mkubwa na upole na uvumilivu, mkichukuliana kila mmoja katika upendo

"jifunzeni kuwa wanyenyekevu, wapole, waumilivu na kuchukuliana kila mmoja katika upendo"

Tunzeni umoja wa Roho katika kifungo cha amani

"tafuteni kuishi pamoja kwa amani kuuhifadhi umoja wa Roho"

Ephesians 4:4

Mwili mmoja

Kanisa mara nyingi linatafasiriwa kama mwili wa Kristo.

Roho moja

"Roho Mtakatifu mmoja tu" (UDB)

Pia mliitwa katika ujasiri wa taraja moja

"Mungu aliwachagua ninyi katika tumaini moja la uhakika"

Baba wa wote ... juu ya wote ... na katika yote ...na ndani ya wote

"Baba wa kila kitu...juu ya kila kitu...kupitia kila kitu...katika kila kitu"

Ephesians 4:7

kauli unganishi

Paulo anawakumbusha waamini juu ya karama ambazo Kristo huwapa waamini kutumia katika kanisa ambalo ni mwili wote wa waamini.

maelezo ya jumla

Nukuu hii imetoka katika wimbo mfalme Daudi aliimba.

Kwa kila mmoja wetu amepewa karama

Hii yaeza elezwa kwa kutumia kauli tendaji. "Mungu ametoa karama kwa kila mmoja wetu" au "Mungu alitoa karama kwa kila muumini"

Alipopaa juu sana

"wakati Kristo alipokwenda juu mbinguni"

Ephesians 4:9

Alipaa

"Kristo alikwenda juu"

Pia alishuka

"Kristo alishuka pia"

Pande za chini za dunia

Yaweza kumaanisha kwamba 1) "katika maeneo ya chini, ya dunia" au 2) "katika sehemu za chini, za dunia."

Aweze kuvijaza vitu vyote

"iliaweze kuwa kila mahali kwa nguvu zake"

jaza

"kamilisha" au "kuridhisha"

Ephesians 4:11

Kristo alitoa karama kama hizi

"Kristo alitoa karama kwa kanisa kama hizi"

kuwawezesha waamini

"kuwaanda waamini" au "kuwapatia waamini"

Kazi ya huduma

"kuwahudumia wengine"

Kwa ajili ya ujenzi wa mwili wa Kristo

Hii inalinganishwa ukuaji wa kiroho kwa kufanya mazoezi kuongeza nguvu ya mwili wa binadamu."

kuujenga

"uboreshaji"

mwili wa Kristo

"mwili wa Kristo" wa husu waumini mmoja mmoja wa mwili wa Kristo.

Kuufikia umoja wa imani na maarifa ya mwana wa Mungu

Maarifa ya Yesu Kristo kama mwana wa Mungu ni ya mhimu katika kuufikia umoja wa imani na ukomavu kama waamini.

Kufikia umoja wa imani

"kuwa na usawa wa nguvu katika imani"

Mwana wa Mungu

Hiki ni cheo mhimu cha Yesu.

Kuwa wakomavu

AT: "Kuwa waamini waliokomaa"

mkomavu

"mtu mzima," "amekuwa," au "mkamilifu"

Ephesians 4:14

Kuwa kama watoto

Hii ni kulinganisha waamini ambao hawajakuwa kiroho na mtoto ambaye amekuwa na udhoefu mdogo sana katika maisha."

Kurushwarushwa na kuchukuliwa huku na huku na kila upepo wa fundisho

Hii inamlinganisha muumini ambaye hajakomaa na husikia fundisho potofu na boti ambayo inarushwa na upepo katika mwelekeo usio sahihi juu ya maji.

Kwa hila ya watu katika ujanja wa udanganyifu uliopotoka

"kwa watu wajanja ambao hupotosha waamini kwa uongo wa kiujanja"

Katika yeye aliye kichwa...mwili wote hukua na kujengeka wenyewe juu

Paulo anatumia mwili wa binadamu kuelezea namna gani Kristo husababisha waamini kfanya kazi pamoja katika umoja kama kichwa cha mwili husababisha sehemu za mwili kufanya kazi pamoja ili kukuwa kiafya.

pamoja na kila kiungo

"kiungo" ni ukanda madhubuti unao unganisha mifupa katika mwili.

Ili kwamba mwili wote ukue na kujijenga wenyewe juu katika upendo

"Hivyo, waamini wanaweza kusaidiana kila mmoja na mwenzake kukua katika upendo"

Ephesians 4:17

Sentensi unganishi:

Paulo anawaambia wao kile ambacho hawapaswi kufanya sasa tu kwasababu wao kama waamini wamewekewa mhuri na Roho Mtakatifu wa Mungu.

Hivi nasema kwahiyo, na ninawasihi ninyi katika Bwana

"Kwahiyo, ninawatia moyo kwa nguvu katika Bwana"

Msitembee tena kama wamataifa wanavyotembea katika ubatili wa akili zao

"Acheni kuishi kama wamataifa na fikra zao zisizonamaana"

Kutiwa giza katika fikra

Hawawezi kufikiri au kuhoji kwa usahihi.

kufukuzwa kutoka katika maisha ya Mungu kwa ujinga uliomo ndani yao na kwa ugumu wa mioyo yao

"Hawawezi kuhisi maisha ya Mungu kwa sababu akili zao zimepofushwa na ni wagumu"

Kufukuzwa

"kukatiliwa mbali" au "kutengwanisha"

ujinga

"ukosefu wa maarifa" au "ukosefu wa taarifa"

sababu ya ugumu wa mioyo yao

Wamekataa kumsikiliza Mungu na kufuata mafundisho yake.

wamejikabidhi wenyewe kwa ufisadi katika matendo machafu

Paulo anawaongelea awa watu kama wao ni vitu wanaojikabidhi wao wenyewe kwa watu, na anaongelea jinsi wanavyo taka kuridhisha tamaa zao za mwili kana kwamba ndio mtu wanao jikabidhi kwake. "Wanacho taka tu nikuridhisha tamaa zao za mwili"

jikabidhi

"kujitoa kabisa"

Ephesians 4:20

Lakini hivi sivyo mlivyojifunza kuhusu Kristo

"Lakini hamkujifunza kumfuata Kristo kwa namna hii"

Kama mmesikia kuhusu yeye na mmefundishwa katika yeye, kama ilivyo kweli iliyo ndani ya Yesu

"Kwavile mmesikia kuhusu Yesu na mmejifunza ukweli kuhusu yeye"

Ninyi lazima mvue utu wa kale- ule ambao unakubaliana na tabia zenu za kale, ambao umeharibika sawasawa na tamaa za udanganyifu

AT: "Ninyi lazima mziondoe tabia ambazo zilikuwa za kawaida kwa njia za maisha yenu ya kale, ambazo zilikuwa mbaya kama tamaa zenu mbaya zilivyowadanganya ninyi"

Lazima muuvue utu wa kale

Lazima mwachane na tabia zote za dhambi kama tu kuvua nguo na kuzitupa mbali. AT: "Lazima mbadili tabia zenu."

Zile zinazoendana na mwenendo wenu wa kale

AT: "tabia ambazo zinakubaliana na asili yenu ya kale" au "tabia ambazo zinakubaliana na ukale wenu"

Ambayo imeharibiwa kulingana na tamaa danganyifu

AT: "ambayo inaendelea kukua vibaya kwasababu ya tamaa za mwili zidanganyazo"

Ephesians 4:23

vueni utu wenu wa zamani

Paulo anazungumzia tabia njema kana kwamba ni vipande vya nguo. "Lazima ubadili tabia" au Lazima uweke mbali mtu wa kale"

mfanywe upya katika roho ya akili zenu

Hii ya weza badilishwa katika njeo tendaji. "Mungu anaweza kukusaidia ukuwe karibu na yeye na kufikiri kwa namna mpya"

Ili kwamba mweze kuvaa utu mpya

Mtu asiye mwamini anakuwa mtu mpya anapokuwa muumini katika Kristo kama ilivyo kwa mtu anavyovaa nguo mpya na kuonekana tofauti kabisa.

unaoendana na Mungu

" inayo akisi tabia ya Mungu" au "yenye kuonyesha jinsi Mungu alivyo"

Ephesians 4:25

Wekeni mbali uongo

"Lazima mwache kusema uongo"

Mnene ukweli, kila mmoja na jirani yake

"Waamini lazima wanene ukweli kwa majirani zao"

Sisi ni wajumbe kila mmoja kwa mwingine

"Sisi sote ni wajumbe wa familia ya Mungu"

Mwe na hasira, lakini msitende dhambi

"mnaweza kukasirika, lakini msitende dhambi"

Msiliruhusu jua kuzama mkiwa na hasira zenu

"Lazima mwache kuwa na hasira kabla usiku haujaingia" au "muiondoe hasira yenu kabla ya siku haijaisha"

msimpe ibilisi nafasi

"Msimpe ibilisi fursa ya kukupeleka dhambini"

Ephesians 4:28

Kauli mbaya isitoke kinywani mwenu

"msiruhusu lugha mbaya itoke kinywani mwenu" au "msiruhusu mazungumzo maovu yatoke kinywani mwenu"

Badala yake maneno ambayo ni msaada kwa kuwajenga wengine

"badala yake neneni maneno ambayo ni msaada katika kutoa afya kwa waamini wengien"

Kuwapa neema wao ambao wanasikiliza

"kwa njia hii mtatoa neema kwa wale ambao wanasikiliza"

faida

"saidia" au "msaada"

Msimhuzunishe

"msitese" au "msiudhi"

Kwa yeye ambaye mmewekewa mhuri kwa ajili ya siku ya ukombozi

Paulo anasema Roho Mtakatifu amewaakikishia waamini kuwa Mungu atawapatia ahadi aliyo waahidi. Roho ni kama alama ambayo Mungu amewaekea watu wake kuonyesha kuwa anawamiliki. "Ni Roho ambaye Mungu amekupa kuonyesha kuwa anakumiliki na ata kukomboa kwa wakati muafaka"

Ephesians 4:31

sentensi unganishi

Paulo anamaliza maelekezo ya kuhusu yapi waamini wasifanye na anamaliza na yapi wafanye.

lazima muweke mbali

tafsiri zilizopo ni 1) lazima ufanye mwenyewe au 2) "lazima umuruhusu Mungu aondoe"

weka mbali uchungu wote

"acha kuwa na hasira ya mambo mabaya watu walio kufanyia"

ghadhabu

wakati wa hasira nzito

hasira

neno lililo zoeleka la hasira

mwe na huruma

" badala yake, lazima uwe na huruma

msameheane

"upole" au "huruma sana"

Ephesians 5

aefeso 05 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Baadhi ya tafsiri huweka kila mstari wa mashairi upande wa kulia zaidi kuliko maandiko yote ili iwe rahisi kusoma. ULB inafanya hivi kwa maneno ya mstari wa 14.

Dhana maalum katika sura hii

Urithi wa ufalme wa Kristo

Hii ni vigumu kuelewa. Baadhi ya wasomi wanaamini kuwa wale wanaoendelea kufanya mambo haya hawataurithi uzima wa milele. Lakini Mungu anaweza kusamehe dhambi zote zilizotajwa katika aya hii. Kwa hiyo washerati, wasio wasafi, au wenye tamaa wakingali wanaweza kupata uzima wa milele ikiwa wanatubu na kumwamini Yesu. Somo la asili zaidi ni "Hakuna mtu ambaye ni mzinzi au msherati, au mlafi (kwani hii ni sawa na kuabudu sanamu) atakayekuwa kati ya watu wa Mungu ambao Kristo anatawala kama mfalme." (UDB) (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#forgive, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#eternity and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#life and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#inherit)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Wanawake, watii waume zenu

Wasomi wamegawanywa juu ya jinsi ya kuelewa kifungu hiki katika mazingira yake ya kihistoria na ya kitamaduni. Baadhi ya wasomi wanaamini kama wanaume na wanawake ni sawa kabisa katika mambo yote. Wasomi wengine wanaamini kama Mungu aliumba wanaume na wanawake kutekeleza majukumu tofauti katika ndoa na kanisa. Watafsiri wanapaswa kuwa makini wasiweke jinsi wanavyoelewa suala hili kuathiri jinsi wanavyotafsiri kifungu hiki.

<< | >>

Ephesians 5:1

Kauli unganishi

Paulo anaendelea kuwaambia waumini jinsi wanavyotakiwa na wasivyotakiwa kuishi kama watoto wa Mungu.

Kwa hiyo mwe wa kumuiga Mungu

"Hivyo ninyi mfanye mambo ambayo Mungu hufanya"

kama watoto wake wapendwa

Mungu anatamani sisi tumuige yeye maadam sisi ni watoto wake.

tembea katika upendo

"ishi maisha ya upendo"

sadaka na dhabihu, harufu nzuri inayompendeza Mungu

"sadaka inayonukia vizuri na dhabihu kwa Mungu"

Ephesians 5:3

uovu wa kujamiiana au uchafu au tamaa ya anasa lazima usidokezwe kati yenu, kama ilivyo sahihi kwa waumini

"siruhusu hata mawazo ya uovu wa kujamiina au uchafu au urafi kupatikana kati ya watu wa Mungu"

uchafu wowote

"maadili yoyote yasiyosafi"

kupenda anasa kwa ulafi

NI: "kutamaa kwaajili ya walivynavyo wengine"

kama ilivyosawa kwaajili ya waumini

NI: "tabia zenu daima ziwe zinazofaa kama watu watakatifu wa Mungu"

lazima usidokezwe kati yenu

"lazima usitajwe kati yenu" au "lazima usigundulike kati yenu"

Ephesians 5:5

urithi

Kupokea kile Mungu alicho ahidi waamini ni mfano wa mtu kurithi mahali au utajiri kwa familia.

matupu

"Msiruhusu mtu yeyote awadanganye kwa hoja za uongo" au "Msiruhusu mtu yeyote awakoseshe ninyi kwa maneno yasiyokuwa na maana"

Ephesians 5:8

Hapo kale ulikuwa giza

Kama tu mmoja hawezi kuona gizani, ndivyo watu wanaoishi katika dhambi wanapungukiwa ufahamu wa kiroho.

Lakini sasa ninyi ni nuru katika Bwana

Kama tu mmoja anaweza kuona katika nuru, ndivyo watu ambao wanaishi katika haki wanaufahamu wa kiroho.

kwa sababu tunda la haki ni uzuri wote, haki, na kweli

kazi zinazotoka kwenye maisha ya muumini (uzuri, haki, na kweli) zinafanana na tunda zuri linalozalishwa na mti wenye afya.

hazina ushirikiano pamoja na kazi zisizozaa za giza

"Usijihusishe na kazi za dhambi au wasioamini"

kazi zisizozaa za giza

kazi za mtu fulani anayeishi katika giza la kiroho zinafanana na matendo maovu ya watu wanaofanya kazi za uovu wamefichwa na giza usiku.

lakini afadhali uwafichue

"lakini heri uwaweke wazi kuwa wanamakosa"

Ephesians 5:13

sentensi unganishi

Haijulikani kama nukuu hii ni zile za Nabii Isaya au ni nukuu ya nyimbo zilizoo imbwa na waamini.

Kila kitu kimefunuliwa na nuru

Kama vile nuru hufunua vitu ambavyo vilikuwa vimefichwa katika ulimwengu unaoonekana, hivyo nuru ya Kristo inafunua uovu wa matendo ya kiroho ya wasioamini katika ulimwengu wa kiroho.

Amka, wewe uliyelala, na inuka kutoka kwa wafu

Wasioamini wanahitaji kuamka kutoka katika kifo cha kiroho kama vile mtu ambaye amekufa lazima afufuke tena ili kusudi aitikie.

wewe ulalaye ... atang'aa juu yako

"wewe" ya husu "aliyelala"

Kristo ataangaza juu yako

Kristo atamwezesha asiyeaamini kufahamu kiasi cha msamaha kilichotolewa na maisha mapya kama vile nuru inavyoonesha dhahiri kilichoko pale ambacho kilikuwa kimefichwa na giza.

Ephesians 5:15

Hivyo basi uwe makini jinsi mnavyoishi, siyo kama watu wasio na hekima bali kama wenye hekima

Wasio na hekima hawajilindi wenyewe kinyume na dhambi. Kwa hali yoyote watu wenye hekima wanaweza kutofautisha dhambi na kuikimbia. NI: "Hivyo basi ni lazima muwe makini muishi sawa na watu wenye hekima zaidi kuliko mtu mpumbavu" au "Hivyo basi lazima mwe makini kuishi sawasawa na mtu mwenye hekima."

Komboa wakati

Tunalo chaguo la kuishi katika dhambi ambalo ni sawa kama kutumia wakati wetu bila hekima. Au tunaweza kuishi tukifanya ambacho Bwana anataka sisi tufanye na kuutumia muda wetu kwa hekima. KWAMBA: "Tumia muda wako kwa hekima."

kwasababu siku ni mbaya

Neno "siku" linamaanisha ni katika muda unaoishi

Ephesians 5:18

sentensi unganishi

Paulo anamaliza maelekezo yake kwa jinsi gani waamini wapswa kuishi.

Na usilewe kwa mvinyo

"Na usilewe kutokana na kunywa mvinyo"

badala yake uwe umejaa na Roho Mtakatifu

"badala yake uwe uliyejaa na Roho Mtakatifu"

katika zaburi na sifa na nyimbo za kiroho

"pamoja na aina zote za nyimbo za kumsifu Mungu"

daima mkitoa shukrani

"Mtoe shukrani daima"

mkijitoa wenyewe

"Kwa unyenyekevu jitoeni wenyewe"

Ephesians 5:22

sentensi Unganishi:

Paulo anatoa maelekezo kwa mume na wake juu ya jinsi wanavyopaswa kutendeana.

yeye ni mwokozi wa mwili

NI: "Kristo ni Mwokozi wa mwili wa waumini" au "Kristo ni Mwokozi wa waumini wote"

Hivyo pia wake wawe kwa waume zao katika kila kitu

NI: "hivyo wake lazima pia wawe watiifu kwa waume zao katika kila jambo"

Ephesians 5:25

wapendeni wake zenu

Hapa "pendo" linarejea pasipo ubinafsi, kutumika, au kutoa upendo.

kujitoa mwenyewe kwaajili yake, kwamba unaweza kumfanya yeye mtakatifu kwasababu yeye alitusafisha sisi

Maneno "mwenyewe" na "yeye" yanarejea kwa Kristo. Maneno "yeye" na "sisi" yanarejea kwa Kanisa.

kajitoa mwenyewe kwaajili yake

NI: "Kristo alitoa kila kitu kwaajili yake"

yeye alitusafisha sisi kwa kutuosha kwa maji kupitia neno

Maana zinazowezekana ni 1) Paulo anarejea kuwa umekuwa ukisafishwa kwa neno la Mungu na kupitia ubatizo wa maji katika Kristo au 2) Paulo anasema Mungu alitufanya sisi wasafi kiroho kutoka katika dhambi zetu kwa neno la Mungu kama tunavyoifanya miili yetu safi kwa kuiosha kwa maji.

kwamba yeye aweza kujiwasilishia mwenyewe kanisa

"kwamba anaweza kuwasilisha kwake mwenyewe kanisa"

bila waa au kunyanzi

Paulo anasema kuhusu Kanisa kama vazi ambalo ni safi na liko katika hali nzuri. Anatumia wazo lile lile katika namna mbili kusisitiza utakatifu wa Kanisa.

takatifu na bila makosa

Kauli "bila makosa" kimsingi inamaanisha kitu kile kile "mtakatifu." Paulo anatumia viwili pamoja kusisitiza utakatifu wa kanisa.

Ephesians 5:28

kama miili yao wenyewe

NI: "kama wapendavyo miili yao wenyewe"

badala yake anaurutubisha

"badala yake anautunza" au "yeye anaulinda"

sisi tu viungo vya mwili wake

Inawezekana ikamaanisha 1) "sisi ni jumuiya ya mwili wake" au 2) waumini wanashikamana kuutengeneza mwili wa Kristo kama vile viungo vya mwili wa mwanadamu vinavyoshikamana kuunda mtu.

Ephesians 5:31

kwa kisababishi hiki

"kwa sababu hii"

lazima kumpenda mke wake kama yeye mwenyewe

Maneno haya "yeye" na "mwenyewe" yanarejea kwa mwanaume muumini ambaye kaoa.

mke lazima amheshimu mume wake

"mke lazima amtii mume wake"

Ephesians 6

Waefeso 06 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Utumwa

Paulo hajaandika katika sura hii ikiwa utumwa ni nzuri au mbaya. Paulo anafundisha kuhusu kufanya kazi ili kumpendeza Mungu ukiwa mtumwa au bwana. Anachofundisha Paulo hapa juu ya utumwa kingekuwa cha kushangaza. Katika wakati wake, mabwana hawakutarajiwa kuwaheshimu watumwa wao na kutowatisha.

Mifano muhimu ya matamshi katika sura hii

Silaha za Mungu

Mfano hii inaelezea jinsi Wakristo wanaweza kujikinga wakati wanavamiwa kiroho. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#spirit and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

__<< | __

Ephesians 6:1

sentensi unganishi

Paulo anatoa maelekezo kwa watoto, wababa, wafanya kazi, na mabwana.

Watoto watiini wazazi wenu katika Bwana

Paulo anarejea kwa watoto kuwatii wazazi wao wa kimwili.

Ephesians 6:4

Na ninyi akina baba msiwakwaze watoto na kuwasababishia hasira

"Ninyi wababa msifanye mambo ambayo yatawafanya watoto wenu wakasirike" au "Ninyi akina baba msiwasababishie wattoto wenu kuwa na hasira"

muwalee katika maonyo na maagizo ya Bwana

"wasaidieni kukua katika mafunzo na mafundisho ya Bwana"

Ephesians 6:5

watumwa, iweni watiifu kwa

"Ninyi watumwa mnapaswa kutii"

kwa heshima kubwa na kutetemeka

Hizi ni njia mbili zinazofanana kuonyesha heshima kuhusu mabwana zao.

kutetemeka kwa hofu itokayo mioyoni mwenu. Tiini kama vile mnavyomtii kristo

"Nyeyekeeni kwa hofu, kama kumtii kristo"

usiwe tu pale mabwana zenu wanapowatazama

"siku zote fanya kazi kama ulivyokuwa ukifanya kazi kwa ajili ya kristo mwenyewe, hata kama mabwana zenu hawawatazami"

kama watumwa wa Kristo

watumikieni mabwana zenu ingawa bwana wenu duniani ni Kristo.

Watumikieni kwa mioyo yenu yote. Kana kwamba kumtumikia Bwana na wala si wanadamu

"fanya kwa furaha maana unafanya kwa ajili ya Bwana na si kuwafurahisha wanadamu."

Ephesians 6:9

fanyeni vivyo hivyo kwa watumwa wenu, na msiwatishie

Msiwatishie watumwa wenu, lakini muwafundishe kama Kristo angeweza kuwafundisha"

mkijua kwamba yeye aliye Bwana wa wote ni yule aliye mbinguni

"kwa sababu mnajua kuwa Krisato ni Bwana wa wote watumwa na Mabwana zao"

Mkijua kuwa hakuna upendeleo kwake

"Na hana upendeleo"

Ephesians 6:10

sentensi unganishi

Paulo anatoa maelekezo kuwafanya waumini kuwa na nguvu katika hii vita tunaishi kwa ajili ya Bwana.

iweni na nguvu katika Bwana na katika uwezo wa nguvu zake

"Hii inategemea kikamilifu katika Bwana kuwapa nguvu ya ya Kiroho"

Vaeni silaha zote za Mungu zilizo kamili, ili kwamba mpate kusimama kinyume na hila za shetani

Wakristo wanapaswa kutumia raslimali zote ambazo Mungu amewapa ili kusimama kinyume na shetani kama vile maaskari wa wanavyoweka siraha za kujikinga mwenyewe kutoka kwa uvamizi wa maadui.

Ephesians 6:12

damu na nyama

Hii fafanuzi inahusiana na watu, siyo roho ambazo hazina mwili wa Binadamu.

kwa hiyo, vaeni silaha zote za Mungu

wakristo wanapaswa kutumia raslimali za kukinga ambazo Mungu amewapa katika kupigana na shetani kwa njia ile askari hubeba silaha ili kujilinda dhidi ya maadui.

Ephesians 6:14

hatimaye simameni imara

maneno "simameni imara" ni lugha yenye maana ya "kuzuia vikali"

mkanda wa kweli

kweli inashika kila kitu pamoja kwa ajili ya muumini kama mkanda unavyoshika nguo zote za askari pamoja.

haki kifuani

Zawadi ya haki inafunika mioyo ya waumini kama kitu cha kulinda kifuaniani kwenye kifua cha Askari.

mkiwa mmevaa utayari miguuni mwenu ili kutangaza injili ya ya Amani

Ni askari pekee anavaa ili kumpa maalifa ya kutembea, muumini anapaswa kuwa na maarifa imara ya injili ya amani ili kuwa tayari kuitangaza.

kila hali mkichukua ngao ya Imani

Imani ambayo Mungu amempa muumini ni lazima itumike kwa ajili ya ulinzi wakati shetani anapovamia kama vile ngao ambayo askari anaitumia kujikinga kutoka katika uvamizi wa maadui.

kuizima mishale ya mwovu Ibilisi

Uvamizi wa shetani katika kumvamia muumini ni kama mishale ya moto inayorushwa kwa askari na adui.

Ephesians 6:17

Na mvae kofia ya wokovu

Wokovu uliopewa na Mungu unalinda mawazo ya muumini kama vile kofia inavyolinda kichwa cha askari.

na upanga wa Roho, ambayo ni neno la Mungu

Neno la Mungu, limevuviwa na Roho Mtakatifu, ili litumike kwa kupigana kinyume na kuwalinda waumini kutoka kwa mwovu kama vile askari anavyotumia upanga kupigana na kujilinda dhidi ya adui anayevamia.

pamoja na kusali na kuomba, ombeni kwa Roho

"Ombeni wajati wote katika Roho kama unavyoomba na ufanye maombezi maalumu"

kwa uvumilivu wote na maombi kwa ajili ya waumini wote

"Mara kwa mara tuwe macho kwa kuomba kwa ajili ya waumini wote"

Ephesians 6:19

sentensi unganishi

Paulo anawaomba kuomba kwa ajili ya ujasiri wake katika kusema injili wakati akiwa gerezani na akasema anamtuma Tikiko ili kuwafariji. Kisha alitoa baraka za amani na neema kwa waumini wote wanaompenda Yesu.

ili niweze kupewa ujumbe

"Kwamba Mungu anipe neno" au "Mungu atanipa ujumbe"

ninapofungua mdomo wangu ili kuufanya ujulikane kwa ujasiri

"Ninapoongea kufafanua kwa ujasiri"

kwa sababu hii mimi ni balozi niliyefungwa minyororo

Niko gerezani sasa kwa sababu ya kuwa mwakilishi wa Injili"

kwamba katika kifungo changu niseme kwa ujasiri kama ninavyowiwa kusema

"Kwamba niseme ujumbe wa Mungu kwa ujasiri wakati nikiwa humu gerezani"

Ephesians 6:21

mambo yangu

"Yaliyonipata" au "Hali yangu"

Tikiko

Tikiko alikuwa ni mmoja wa watu waliokuwa wakitumika na Paulo.

atawajulisha kila kitu

"Atawaambia kila kitu"

Ephesians 6:23

Sentensi unganishi

Paulo anafunga barua yake kwa wa Efeso na baraka ya amani na neema kwa wote waamini wanao mpenda Kristo.

Utangulizi wa Wafilipi

Sehemu ya 1: Utangulizi wa jumla

Muhtasari wa kitabu cha Wafilipi

  1. Salamu,kushukuru na sala (1:1-11)

  2. Ripoti ya Paulo kuhusu huduma wake (1:12-26).

  3. Maelekezo

  4. Timotheo na Epafrodito (2:19-30)

  5. Onyo kuhusu walimu waongo (3:1-4:1)

  6. Maagizo ya kibinafsi(4:2-5)

  7. Uwe na furaha na usiwe na wasiwasi (4:4-6)

  8. Maneno ya mwisho

Nani aliandika kitabu cha Wafilipi?

Paulo aliandika Wafilipi. Paulo alitoka katika Mji wa Tarso. Hapo awali alijulikana kama Saulo. Alikuwa Mfarisayao kabla hajakuwa Mkristo. Aliwatesa sana Wakristo. Baada ya kuwa Mkristo, alisafiri sehemu nyingi katika ufalmwe ya Warumi akiwaambia watu kumhusu Yesu.

Paulo aliandika barua hii akiwa gerezani pale Roma.

Kitabu cha Wafilipi kinahusu nini?

Paulo aliwaandikia barua hii Waumini wa Filipi, mji ulioko Makedonia. Aliiandika kuwashukuru Wafilipi kwa zawadi waliomtumia. Alitaka kuwaelezea hali yake gerezani na kuwahimiza kuwa na furaha hata kama walikuwa wanateseka. Aliwaandikia pia kumhusu mtu mmoja aliyeitwa Epafrodito.Yeye ndiye aliyemplekea Paulo zawadi. Wakati akimpelekea zawadi, Epafrodito akawa mgonjwa.Kwa hivyo Paulo akaamua kumrudisha nyumbani Filipi. Paulo aliwahimiza waumini wa Filipi kumkaribisha na kumfanyia wema Epafrodito atakaporudi.

Kichwa cha kitabu hiki kinastahili kitafsiriwe namna gani?

Watafsiri wanaweza kukiita kitabu hiki jina lake la jadi,"Wafilipi." ama wanaweza kutumia kichwa kinachoeleweka zaidi kama "Barua ya Paulo kwa Kanisa la Filipi." ama "Barua kwa Wakristo walioko Filipi." (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-names).

Sehemu ya 2: Maswala muhimu ya Kidini na Kitamaduni

Mji wa Filipi ulikuwa namna gani?

Filipi, baba yake Alekzanda Mkuu ndiye aliyeuanza mji wa Filipi katika eneo la Makedonia. Hii inamaanisha kwamba raia wa mji wa Filipi walichukuliwa kama raia wa Roma. Lakini Paulo akawaambia kwamba walikuwa raia wa mbinguni (3:20).

Sehemu ya 3: Maswala muhimu ya tafsiri

Umoja na wingi wa "nyinyi"

Kwenye kitabu hiki, Paulo anatumia neno "mimi' kumaanisha yeye. Neno "nyinyi" limetumika kama wingi na kumaanisha waumini wa Filipi. Mahali tu hii haizingatiwi ni 4:3(Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-exclusive and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-you).

Nani walikuwa "Maadui wa Msalaba wa Kristo" (3:18) katika barua hii?

Pengine "Maadui wa msalaba wa Kristo" walikuwa watu waliojiita waumini lakini hawakufuata maagizo ya Mungu. Walifikiri kwamba uhuru ndani ya Kristo ilimaanisha kwamba Waumini walikuwa huru kufanya wapendalo bila Mungu kuwaadhibu (3:19).

Ni kwa nini maneno "furahi" na "shangwe" yametumiwa mara nyingi katika barua hii?

Paulo alikuwa gerezani wakati aliandika barua hii (1:7). Ingawa alikuwa anateseka, Paulo alisema mara nyingi kwamba alifurahi kwamba Mungu alimpa wema kwa njia ya Kristo. Alitaka kuwahimiza wasomaji wake wawe na tumaini sawa na hilo kwa Yesu Kristo. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-irony)

Paulo anamaanisha nini kwa kauli "ndani ya kristo," "ndani ya Bwana," na kadhalika?

Aina hii ya maelezo inatokea katika 1:1,8,13,14,26, 27;2:1, 5, 19, 24, 29; 3:1, 3,9,14; 4:1,2, 4,7,10, 13, 19, 21. Paulo alitaka kuzungumzia hali ya Yesu kuwa karibu sana na waumini. Tazama utangulizi wa kitabu cha Warumi kwa maelezo zaidi.

Ni mambo gani muhimu zaidi katika maandishi ya kitabu cha Wafilipi?

(See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/jit.html#translate-textvariants)

Philippians 1

Wafilipi 01 Maelezo kwa ujumla

Muundo na mpangilio

Paulo anajumuisha sala mwanzoni mwa barua hii. Wakati huo viongozi wa kidini walianza barua zao zisio rasmi na sala.

Dhana Maalum katika sura hii

Siku ya Kristo

Labda inaashiria wakati Kristo atakaporudi. Paulo aliunganisha kurudi kwa Kristo kwa kutia nia ya kuishi maisha ya kumcha Mungu.

Tafsiri zingine zenye utata katika sura hii

Kitendawili

Kitendawili ni kauli ya ukweli inayaonekana kuelezea kitu kisichowezekana. Kauli hii katika mstari wa 21 ni kitendawili "Kufa ni faida." katika mstari wa 23, Paulo anaelezea ni kwa nini huu ni ukweli. (Wafilipi 1:21).

| >>

Philippians 1:1

Sentensi unganishi

Mwandishi anatoa salamu kwa watu wa kanisa la Filipi

Maelezo ya jumla

Kwa sababu Paulo anaandika baadaye katika barua akisema "mimi," linaleta maana kwamba Paulo ndiye mwandishi na kwamba Timotheo ndiye alikuwa pamoja naye. Na maneno yote ya "wewe" na "ninyi" katika barua hii yanaongelea wakristo wa kanisa la Filipi katika wingi wao. Na neno "yetu" pengine linamaanisha wakristo wote akiwemo Paulo, Timotheo na wakristo wa Filipi.

Paulo na Timotheo

kama lugha yako ina njia maalumu ya kutambulisha waandishi wa barua, itumie hapa.

Timotheo, watumishi wa Yesu

"Timotheo. Sisi ni watumishi wa Kristo Yesu"

Kwa wale walitengwa katika Kristo

"kwa waumini wote katika Kristo Yesu"

waangalizi na wahudumu

" wazee wa Kanisa"

Philippians 1:3

Ninawashukuru kwa ushirika wenu katika injili

Paulo anamshukuru Mungu kwamba wafilipi wnahubiri injili pia. "Ninamshukuru Mungu kwamba mnatangaza injili"

Ninaujasiri

Ninauhakika

Yeye aliyeanza

"Mungu aliyeanza"

Philippians 1:7

Ni haki kwangu

"ni sahihi kwangu" au "ni vizuri kwangu"

nimewaweka moyoni wangu

"ninawapenda sana"

mmekuwa washirika wenza wa neema

"mmefanyika washiriki wa neema pamoja nami" au "kushiriki katka neema pamoja"

Mungu ni shahidi wangu

"Mungu anajua" au "Mungu anafahamu"

katika undani wa huruma ya Kristo Yesu.

Kirai "katika undani wa huruma" inaweza kutafsiriwa pamoja na kitenzi "upendo." "na ninawapenda kama Yesu Kristo alivyotupenda mno sisi sote"

Philippians 1:9

sentensi unganishi

Paulo anawaombea wakristo wa Filipi na kuzungumzia juu ya furaha iliyo katika mateso kwa ajili ya Bwana.

Paulo anazungumzia upendo kana kwamba kulikuwa na upinzani watu wangeweza kupata zaidi. iongezeke"

Katika maarifa na ufahamu wote

Hapa "ufahamu" maana yake ni Mungu kuweza kuwa wazi. "kama ujifunzvyo na kufahamu zaidi kuhusu nini ambacho kinamtukuza Mungu"

"kwa jinsi "mnavyojifunza na kufahamu kwa uwazi mambo yanayompendeza Mungu. "

Thibitisha

Hii hurejea kupima vitu na kuchukua vile ambavyo ni vizuri. "pima na chunguza"

mambo yenye adili

"kile kinachompendeza Mungu zaidi"

muwe safi pasipokuwa na hatia

Maneno" safi" na " kutokuwa na hatia"kimsingi yanabeba maana ile ile. Paulo anayatumia kwa pamoja ili kukazia usafi wa rohoni. "hali ya kutokuwa na lawama"

Ninyi pia mtajazwa

Paulo anazungumzia waamini kana kwamba walikuwa chombo cha kuwekea kitu amabacho kinaweza kujazwa na matunda. "Ili pia kwamba Yesu Kristo awasababishe kumtii Mungu zaidi na zaidi"

mjazwe na tunda la haki itokayo

Matendo mazuri ya mwamini ambaye Mungu aliyaweka wazi vizuri humfurahisha Mungu kama ambavyo tunda kukua kwenye ni mtamu kwa wale walao. "kuweza kumfurahisha Mungu na watu wengine kwa njia unayoishi sasa kwamba Mungu alikusamehe dhambi zako"

kwa utukufu na sifa ya Mungu

Maana ziwezekanazo ni 1) "Ndipo watamsifu na kumpa Mungu heshima kubwa 2)n"Ndipo watu watamsifu Mungu na kumpa Mungu heshima kubwa kwa sababu ya mambo mazuri waonayo ufanayayo." Hizi tafsiri ya mmoja mmoja inaweza kufanya kuhitajike sentensi mpya.

Philippians 1:12

Maelezo ya Ujumla

Paulo anasema kwamba mambo mawili yametokea kwa sababu ya "maendeleo ya injili": watu wengi ndani na nje waligundua kwa nini yuko gerezani, na Wakristo wengine hawana hofu kuhubiri habari njema.

sasa nataka

hapa neno" sasa" limetumika kuonesha mwanzo mpya wa barua

ndugu

hapa linamaanisha wakristo wenzake, likijumuisha wanaume na wanawake, kwa kuwa wauimini wote katika Kristo ni viungo katika familia moja ya kiroho, pamoja na Mungu, baba yao wa mbinguni.

mambo yaliyotukia kwangu

Paulo anazungumzia muda alipokuwa gerezani. mateso niliyoyapata kwasababu nilikuwa nimewekwa gerezani kwa sababu ya kumhubiri Yesu.

yameifanya injili iendelee sana

"yamesababisha watu wengine kumwamini Yesu"

kifungo changu changu katika Kristo kimejulikana

"Minyororo katika Kristo" ni neno linalosimama badala ya kuwa gerezani kwa ajli ya Kristo. "Kumejulikana" ni mfano kwa "kujulika." "Ilijulikana kwamba nipo katika minyororo kwa ajili ya Kristo"

minyororo yangu katika Kristo imejulikana...walinzi...yeyote mwingine

Hii inaweza kuanza muundo wa utendaji. "walinzi wote wa ikulu na watu wengi katika Rumi wanajua kwamba nipo katika minyororo kwa ajili ya Kristo"

minyororo yangu katika Kristo

Hapa Paulo anatumia kihusishi "katika" kumaanisha "kwa ajili ya." "minyororo yangu kwa ajili ya Kristo" au "minyonyororo yangu kwasababu nafundisha watu kuhusu Kristo"

minyororo yangu

Hapa neno "minyororo" linasimama badala "kifungo. "kifungo changu"

ikulu

Hili ni kundi la maaskari waliosaidia kulinda utawala wa Rumi.

Philippians 1:15

kwa hakika, hata Baadhi yao humtangaza Kristo

"Baadhi ya watu huhubiri habari njema ya Yesu"

kwa wivu na ugomvi

"kwasababu hawapendi watu wanisikilize mimi na wanapenda kusababisha matatizo"

wengine kwa nia njema

"lakini watu wengine hufanya hivyo kwasababu ni wapole na wanapenda kunisaidia"

mwishoni mwa hotuba yake

"Wale ambao wanamtangaza Kristo kwa nia mbaya"

Nimewekwa hapa kwa ajili ya kuitetea injili

Hii inaweza kuanza kwa muundo tendaji. Maana zinazowezekana ni 1) "Mungu amenichagua kuitetea injili" au 2) "nipo gerezani kwa sababu naitetea injili."

kwa ajili ya kutetea injili

"kumhubiri kila mmoja kuwa uhabari za Yesu Kristo ni za kweli"

Bali wengine wamtangaza Kristo

"bali wengine" au "bali mwingine anamuhubiri Kristo nje kwa hila na vita

wakati nipo katika minyororo yangu

Hapa neno "minyororo" linasimama badala ya kifungo. "while nimimefungwa" au "wakati nimefungwa"

Philippians 1:18

ni nini hii?

Paulo anatumia hili swali kuwaambia vile asikiavyo kuhusus hali aliyoandika katika 1:15. maana zaweza kuwa "haijalishi" neno "nitafikiria kuhusu hii" ilieleweka kama sehemu ya swali. "nitajali kuhusu nini?" au "Hivi ndivyo ninavyofikiri kuhusu hii"

katika njia yoyote ile, katika kusudi baya au zuri, Kristo anahubiriwa

"kwa kuwa watu wanamhubiri Kristo, hakuna shida, kama wanafanya hivyo kwa makusudi mazuri au kwa makusudi mabaya"

ninafurahia jambo hilo

"Nina furaha kwasababu watu wanamhubiri Kristo"

nitafurahia

"Nitasherekea" au "nitashangilia"

hili litaleta kufunguliwa kwangu

"kwa sababu watu wanamuhubiri Kristo, Mungu atanitoa kifungoni/ gerezani"

katika kufunguliwa kwangu

maana halisi ya "kufunguliwa," ni nini Mungu atamfungua Paulo kutoka, haiko wazi. maana hizi zinawezekana 1) Paulo alikuwa anarejea kusaidiwa kutoka katika katika hali mbya au 2) Paulo alikuwa narejea wazi wazi kuwa huru mbali na kifungo.

kupitia maombi yenu na msaada wa Roho wa Kristo Yesu

"kwa sababu mnaomba na Roho wa Yesu Kristo inanisaidia"

Roho wa Yesu Kristo

"Roho Mtakatifu"

Philippians 1:20

matarajio yangu ya uhakika na kweli

"hapa maneno " matarajio ya hakika" na "matarajio ya Kweli" yanamaanisha kimsingi jambo lile lile tu. Paulo anayatumia kwa pamoja ili kutilia mkazo kuonesha matarjio ya dhati aliyonayo. "Ninashawishika kwa dhati"

kwa ujasiri wote, kama ambavyo siku zote na sasa, Kristo atainuliwa"

Hii ni sehemu ya matarajio na matumaini ya Paulo. "lakini natarajia na kutumaini kwamba katika ujasiri wote, sasa kama siku zote, Kristo atainuliwa"

"katika ujasiri wote, sasa na siku zote"

"nitakuwa na ujasiri mkubwa sasa, kama siku zote nilivokuwa na"

Kristo atainuliwa kwenye mwili wangu wangu

kifungu hiki cha neno "mwili wangu" ni neno linalosimama badala vile Paulo amefanya kwenye mwili wake. Hii inaweza kuanza muundo tendaji. Yawezekana maana zikawa 1) "Nitamtukuza Kristo kwa kile nifanyacho" 2) "watu watamsifu Kristo kwa sababu ya kile nifanyacho"

Ikiwa ni kwa uzima au kwa kifo

"kama nitaendelea kuishi au nikifa"

Kwa maana kwangu mimi kuishi ni Kristo na kufa ni faida"

"Kwa maana kama nikiendelea kuishi, nitaishi kumtukuza Kristo, na kama nikifa, hiyo itakuwa nzuri.

Philippians 1:22

kama kuishi katika mwili huleta tunda katika kazi yangu

Neno "tunda" hapa limetumika kurejelea matokeo mazuri ya kazi ya Paulo. " kama kuishi katika mwili kuna nipa fursa ya kuwatia moyo watu ili waamini katika Kristo."

inamaana kwamba matunda ya kazi yangu

Neno "tunda" hapa linarejea matokeo mazuri ya kazi ya Paulo. "inamaana kwamba nitaweza kufanya kazi na kazi yangu itazaa matokeo mazuri" au "maana nitakuwa na nafasi zaidi kuwatia moyo watu kumwamini Kristo"

Ninasukumwa katika vitu viwili

Paulo anazungumzia vile ilivo vigumu kwake kuchagua kati ya kuishi na kufa kama vitu vizito vnavyopingana, kama mawe au magogo, vilikuwa vikimsukuma kwenda kinyume katika wakati mmoja. Lugha yako inaweza kupendelea kupinga kuvuta kuliko kusukuma. "nipo ndani ya mvutano. Sijui kama naweza kuchagua kuishi au kufa"

Ninahamu ya kuuacha mwili na kuwa na Kristo

Paulo anatumia tafsida hapa kuonyesha kwamba haogopi kufa. "ningependa kufa kwa sababu nitaenda kuwa na Kristo"

Philippians 1:25

Kwa kuwa nina uhakika juu ya hili

"Kwa kuwa ninauhakika kwamba ni vizuri kwako kwamba ninaenedelea kuishi"

ninajua nitabaki

" Ninajua kuwa nitaendelea kuishi or ninajua kwamba nitabaki katika mwili, yaani sitakufa"

Ili kwamba kwa mimi

"Hivyo basi kwa sababu ya mimi" au "Kwa hiyo basi kwa sababu ya kile nifanyacho"

kwamba mmesimama imara katika roho mmoja...mkishindania imani ya injili kwa pamoja.

Haya mambo mawili vinashirikiana maana moja kusisitiza umuhimu wa umoja.

kushindana pamoja

"kufanya kazi kwa bidii pamoja"

imani ya injili

ina maana ya "kueneza imani ambayo imejengwa juu ya injili ya Kristo" au "kuamini na kuishi kulingana na habari njema inavyotufundisha"

Philippians 1:28

na msitishwe na kitu chochote

hili ni agizo kwa Wakristo wa Filipi kuwa wasiogope kitu chochote.

Hii ni kwao ni ishara ya uharibifu . Bali kwenu ni ishara ya wokovu, kutoka kwa Mungu

"Ujasiri wenu utawaonyesha kwamba Mungu atawaharibu. Pia itawaonyesha kwamba Mungu atawaokoa"

kwa maana mna ugomvi uleule kama mlivyoona na ule mnaosikia ninao hata sasa

Ndiyo maana mmekuwa na ugomvi ua ushindani uleule kama mlivyoona kwangu na kwa sasa mnasikia kuwa bado ninao.

Philippians 2

Wafilipi 02 Maelezo kwa ujumla

Muundo na mpangilio

zimetenganisha mistari ya 6-11. Mistari hii inafafanua mfano wa Kristo. Inafunza ukweli muhimu kumhusu Yesu.

Dhana muhimu katika sura hii

Maelekezo ya matendo

Paulo anatoa maelekezo mengi ya matendo katka sura hii kwa kwanisa ya Filipi.

Tafsiri zingine zenye utata katika sura hii

"Ikiwako chochote"

Inaonekana hii ni kauli ya nadharia ingawa si hivyo kwa vile inaelezea kitu ambacho ni cha ukweli. Mtafsiri anaeza pia kutafsiri 'kwa sababu kuna.

<< | >>

Philippians 2:1

Sentensi Unganishi

Paulo anawashauri waamini kuwa katika hali ya umoja na unyenyekevu na kuwakumbusha mfano wa Kristo.

Ikiwa

"Ninaamini ni kweli"

ikiwa kuna kutia moyo katika Kristo

"kwamba Kristo amewatia moyo"

ikiwa kuna faraja kutoka katika pendo lake

"ikiwa pendo lake limekupa faraja"

ikiwa kuna ushirika wa Roho

"ikiwa una ushirika pamoja na Roho"

ikiwa kuna rehema na huruma

"ikiwa mmezoea matendo mengi ya Mungu ya huruma na rehema"

fanya furaha yangu

Paulo hapa anazungumzia furaha kana kwamba kilikuwa kimiminika kinajazwa kwenye kibebeo. "Kumenisababisha kusifu mno"

Philippians 2:3

Msifanye kwa majivuno au majivuno

"Usijihudumie mwenyewe au kujiona ni bora kuliko wengine"

Kila mmoja asiangalie mahitaji yake mwenyewe, bali pia ajali mahitaji ya wengine

"usiangalia tu kile unachohitaji, bali nini wengine wanahitaji pia"

Philippians 2:5

Muwe na nia moja kama aliyokuwa nayo Kristo

"Kuwa na nia moja ambayo Kristo Yesu alikuwa nayo" au "fikirieni vile ambavyo Kristo Yesu alivyofanya"

hakujali kuwa sawa na Mungu kuwa kitu cha kushikamana nacho

hapa Paulo anazungumzia usawa na Mungu Baba kana kwamba kulikuwa na kitu ambacho Kristo angeweza kushikilia kwenye mikono yake.

alijishusha mwenyewe

Paulo anamzungumzia Kristo kana kwamba alikuwa kitu cha kubebea ili kusema kwamba Kristo alikataa kutenda katika nguvu ya uungu wake katika kipindi huduma yake duniani

Alijitokeza katika mfano wa mwanadamu. Alinyenyekea

"Maneno "alijitokeza...kama" ni lahaja ya "kuwa." "Kuwa mwanadamu, alinyenyekea"

kuwa mtumwa hadi kifo

Paulo hapa anazungumzia kifo katika njia ya umbo. Anayetafsiri naweza kuielewa aidha kama mfano wa eneo (Kristo alipitia kifo) au kama mfano wa mda (Kristo alitii hata mpaka wakati alipokufa).

kifo cha msalaba

"kufa kwenye msalaba"

Philippians 2:9

jina kuu lipitalo kila jina

Hapa "jina" linasimama badala ya cheo au heshima kuu. "cheo ambacho ni juu ya cheo kingine" au "heshima ambayo ipitayo heshima yeyote"

lipitalo kila jina

Jina ni muhimu zaidi, zaidi kusifiwa kuliko jina jingine lolote.

katika jina la Yesu

Yawezekuwa maana hii "wakati kila mmoja anaposikia jina Yesu"

kila goti lipigwe

Hapa "got" inarelea utu wote, na liiname chini ni mfano wa kuinama kwa kuabudu. "kila mtu atamwabudu Mungu"

juu ya ardhi

yamkini maana zikawa 1) sehemu ambayo watu waendayo wakati wafapo au 2) sehemu ambayo mapepo washipo.

kila ulimi

Hapa "ulimi" inarejea kwenye utu wote. "kila mtu" au kila "kiumbe"

kwa utukufu wa Mungu baba

Hapa neno "kwa" linaonyesha matokeo: "na matokeo ambayo watamsifu Mungu Baba"

Philippians 2:12

Sentensi Unganishi

Paulo anawatia moyo Wakristo wa Filipino na kuwaonyesha jinsi ya kuishi maisha ya Kikristo mbele ya wengine na na kuwakumbusha mfano wake.

mpendwa wangu

"wapendwa wangu waamini"

katika uwepo wangu

"wakati nikiwa nanyi hapo"

katika kutokuwepo kwangu

"wakati pasipo uwepo wangu nanyi hapo"

wajibikieni wokovovu wenu

"kuendelea kumtii Mungu"

kwa hofu na kutetemeka

neno "hofu" na "kutetemeka" kimsingi inamaana moja. Paulo anayatumia kusisitiza utakatifu mbele za Mungu" "tetemeka na hofu" au "na utakatifu wa ndani"

wote kunia na kutenda

"Mungu hutenda kwa hiyo basi mtatamani kumtii na kwa hiyo basi mtamtii"

Philippians 2:14

manung'uniko na uaminifu

Paulo anaeleza wazo moja kutumia maneno ya hasi na chanya. "bila kosa kabisa"

watoto wa Mungu bila lawama

"watoto wa mungu bila kubadilika" au mtoto wa Mungu mkamilifu"

kung'aa kama mwanga

Hapa Paulo anawazungumzia waamini kana kwamba walikuwa mwanga waking'aa gizani, kuwasaidia wengine kutafuta njia ya kumheshimu Mungu. " ishi katika nija ya kumheshimu Mungu"

katika dunia

Hapa "dunia" inarejea kila kitu na tabia ambacho hakimwabudu Mungu

uasi na uovu

haya maneno mawili kimsingi ni kitu kimoja. Paulo anayatumia kusisitiza jinsi kizazi kilivyo kiovu. "kiuvo kabisa"

Shikeni sana neno la uzima

Paulo hapa anazungumzia neno la Mungu kanakwamba lilikuwa kitu ambacho kingeweza kushikika.

kutukuza

"kufurahia" au "kuna na furaha"

katika siku ya Kristo

hii inarejea wakati Yesu atakaporudi kuchukua himaya yake na kutawala dunia nzima. "wakati Yesu atakapokuaja"

sikupiga mbio bure wala sikutaabika

Msisitizo "kupiga mbio bure" na "kutaabika bure" hapa inamaanisha kitu kimoja. Paulo ameyatumia haya maneno yote kusisitiza vile alivyofanya kwa bidii kuwasaidia watu kumwamini Yesu. "sikufanya kazi kwa nguvu bila kitu"

mbio

mara chache maandiko yamezungumza kama mwenendo wa kila mmoja. kupiga mbio ni kuishi maisha yanayoshadidiana.

Philippians 2:17

Lakini hata kama ninamiminwa kama sadaka juu ya dhabihu na huduma ya imani yenu, ninafurahi, na ninafurahi pamoja nanyi nyote

Paulo anazungumzia kifo chake kana kwamba kilikuwa ni kifo cha kuteketeza mnyama ambayo mafuta yalimiminwa. Kile Paulo alimaanisha ni kwamba alikuwa tayari kufa kwa ajili ya Wafilipi kama hiyo ingewafanya wamheshimu Mungu. Pia, hii inaweza kuonyesha katika muundo kamili. "Lakini, hata kama Warumi waliamua kunibagua, nitafurahi katika kifo changu kama kifo changu kitafanya imani yenu na utii zaidi kwa kumheshimu Mungu"

vilevile ninyi pia mnafurahi pamoja nami

Maelezo haya mawili kwa pamoja ni alama ya hiyo furaha. " "ninataka mfurahi pamoja nami"

Philippians 2:19

Sentensi unganishi

Paulo anawaambia waumini wa Filipi kuhusu hili wazo la kumtuma Timotheo baada ya mda mfupi na watamtumia Epafradito kama mtu maalumu

Lakini natumaini katika Bwana Yesu

"Lakini, kama Bwana Yesu atapenda, natumaini"

Kwa kuwa sina mwingine aliye na mtazamo kama mimi

"Hakuna mwingine hapa awapendaye kama yeye awapendavyo"

Wengine wote ambao

Hapa memo "wengine" linarejea kwenye kundi la watu Paulo hawezi kusikia anaweza kuwaamini kuwatuma kwa Wafilipi. Pia Paulo anaeleza kuvunjwa moyo na kundi, ambao wangeweza kuondoka, lakini Paulo hawaamini kuhitimisha makusudi yao.

Philippians 2:22

kama mtoto anayemhudumia baba yake, ndivyo alivyotumika pamoja nami

Paulo anamzungumzia Timotheo, ambaye alimtumikia Kristo pamoja na Paulo, kana alikuwa mtoto akimhudumia baba yake. Paulo anasisitiza mahusiano ya baba na mtoto alinayo pamoja na Timotheo katika kumtumikia Mungu.

katika injili

Hapa "injili" inasimama kama kazi ya kuwaambia watu kuhusu Yesu. "katika kuwaambia watu kuhusu injili"

Nina hakika katika Bwana kwamba mimi mwenyewe nitakuja hivi karibuni

"Ninauhakika, kama ni mapenzi ya Bwana, kwamba nitakuja hivi karibuni"

Philippians 2:25

Epafradito

Hili ni jina la mtu aliyetumwa na kanisa la Filipi kumhudumia Paulo gerezani.

mtenda kazi mwenzangu na askari mwenzangu

Hapa Paulo anamzungumzia Epafradito kana kwamba alikuwa askari. Anamaanisha kwamba Epafradito amejifunza na kuamua kumtumikia Mungu, haijalishi ambavyo mambo makubwa yakayomsonga. "muumini mwenzangu ambaye anafanya kazi na kusumbuka pamoja nasi"

na mjumbe wenu kwa ajili ya mahitaji yangu

"na ambaye aletaye ujumbe wenu kwangu na anisaidiaye wakati ninapokuwa mhitaji"

alikuwa na hofu, na alitamani kuwa pamoja nanyi nyote

"alikuwa na hofu na alitaka kuwa nanyi nyote"

huzuni juu ya huzuni

sababu ya huzuni ingeweza kutengenezwa wazi. "huzuni ya kumpoteza kujumlisha na huzuni aliyokuwa nayo kuwa gerezani"

Philippians 2:28

nitaondolewa wasi wasi

"sintoogopa kama nilivyokuwa"

Mkaribisheni Epafradito

"mpokeeni Epafradito kwa furaha"

katika Bwana kwa furaha

"kama muumini mpendwa katika Bwana pamoja na furaha yote"

alikaribia kufa

hapa Paulo anzungumzia kifo kana kwamba kilikuwa ni sehemu ambayo angeweza kwenda.

kufanya kile ambacho hamkuweza kufanya katika kunihudumia

Paulo anzungumzia mahitaji yake kana walikuwa chombo cha kubebea kwamba Epafradito alijazwa vitu vizuri kwa ajili ya Paulo.

Philippians 3

Wafilipi 03 Maelezo kwa ujumla

Muundo na Mpangilio

Katika mistari 4-7, Paulo anaorodhesha jinsi anavyostahili kuitwa Myahudi mwenye haki. Kwa kila namna, Paulo alikuwa Myahudi kamili kabisa. Lakini anatofautisha hii na ukuu wa kumfuata Yesu. (Tazama : https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous)

Dhana muhimu katika sura hii

Mbwa

Watu wa kale wa Mashariki ya Karibu wallitumia taswira ya mbwa kama ishara ya watu kwa njia isiyo pendeka. Siyo mila zote hutumia "mbwa" kwa njia hii.

Miili iliyofufuka

Tunafahamu kwa uchache jinsi watu watakavyokuwa mbinguni. Paulo anafundisha kwamba Wakristo watakuwa na miili ya utukufu na hawatawaliwa na dhambi. (Tazama: //en/tw/dict/bible/kt/heaven and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

Mifano muhimu kwa sura hii

Tuzo

Paulo anatumia mfano endelevu kuelezea maisha ya Kikristo. Lengo la maisha ya Kikristo ni kujaribu kukuwa kama Kristo hadi mtu afariki dunia. Hatuwezi kulifikia hili lengo kikamilivu lakini ni lazima tujitahidi kulifikia.

<< | >>

Philippians 3:1

Sentensi unganishi

ili kuwaonya waumuni wake wapendwa kuhu Wayahudi ambao wangependa kupata kufwata sheria za zamani, Paulo anatoa ushuhuda wake kuhusu ambavyo alivyo watesa waamini.

Hatimaye, ndugu zangu

"Sasa kutembea pamoja, ndugu zangu"

ndugu

neno hili humaanisha Wakristo wenza, ikijumuisha wanaume na wanawake, kwa kuwa waumuni wote katika Kristo ni washiriki wa familia moja ya kiroho, ambayo Mungu ni baba wa mbinguni.

furahini katika Bwana

"kuweni na furaha kwa sababu ya yote Yesu aliyafanya"

usumbufu

kuudhi

haya mabo yatawapa usalama

Hapa "haya mambo" inarejea kwa mafundisho ya Paulo.

kujihadhari

"kuwa makini na" au "kujihadhari kwa"

mbwa...watenda kazi wabaya...pruni

Haya ni maneno matatu tofauti ya kueleza kundi moja la walimu wa uongo. Paulo anatumia maelezo imara kuonyesha hisia zake kuhusu hawa Wayahudi walimu.

Mbwa

Neno "mbwa" lilitumiwa na Wayahudi likimaanisha wale waliokuwa siyo Waisrael.Walitazamwa kama wachafu. Paulo anawalinganisha walimu wa uongo kama tusi. Kama kuna mnyama wingine katika utamaduni wenu anayefikiriwa kuwa mchafu, au anatumiwa kama mchafu, unaweza kutumia mnyama huyu badala yake.

wajikataaokatika miili yao

Paulo anabagua kuhusu kitendo cha tohara kuwatukana walimu wa uongo. Walimu wa uongo wanafundisha Mungu atamwokoa mtu aliyetahiriwa tu, ambaye amekatwa sehemu ya mbele ya ngozi.Hili tendo lilitakiwa lifanyike kwa sheria ya Musa kwa wanaume wote wa Israeli.

Kwa kuwa sisi

Paulo anatumia "sisi" kurejea yeye mwenyewe na waamini wa kweli katika Kristo, pamoja na waamini wa Wafilipi

tohara

Paulo anatumia kirai/kifungu cha maneno kurejea waamini katika Kristo ambao bado hawajatahiriwa katika mwili lakini wametahiriwa katika kiroho, maana yake ni kwamba wamempokea Roho Mtakatifu kupitia imani. "watu wa Mungu wa kweli"

hakuna ujasiri katika mwili

"msiamini kwamba kukata sehemu ya mwili pekee kunaweza kumpendeza Mungu"

Philippians 3:4

Hata hivyo.

"Bado" au "Hata hivyo"

Mimi mwenyewe ningeweza kujivunia mwili. Kama kungekuwa na mtu wa kuutumainia mwili huu, mimi ningeweza kufanya hivyo zaidi.

Hii hali ya kufikirika ambayo Paulo anasema kama ingekuwa inawezekana kuwa Mungu anaokoa watu kwa misingi wa yale waliyofanya, basi Mungu angekuwa kwa uhakika amemuokoa yeye: "Kama yeyote angeweza kuwa amefanya mambo ya kutosha kumpendeza, ingekuwa kuliko mtu yeyote"

Mimi mwenyewe

Paulo anatumia "mimi mwenyewe" kwa kusisitiza. "hakika mimi"

Nilitahiriwa

"Kuhani alinitahiri mimi"

Siku ya nane

"siku saba baada ya kuzaliwa kwangu"

Mwebrania wa Waebrania

"mtoto wa Mwebrania aliye na wazazi wa Kiebrania"

katika kutimiza sheria ni Farisayo

Kama Mfarisayo, "hakika nilijitoa katika sheria"

Philippians 3:6

Kwa juhudi zangu nililitesa Kanisa

Nilidhamiria kuwaumiza waumini wa Kikiristo

kwa kuitii haki ya sheria, sikuwa na lawama kisheria

"Nilitii sheria sheria yote kikamilifu"

mambo yote niliyaona kuwa faida kwangu

hapa Paulo anajea kwenye sifa alizozipata kwa kuwa Mfarisayo mwenye shauku.

Nayahesabu yote kama takataka

Paulo anamalizia kwamba matendo yake ya haki katika dini yalikuwa bure mbele Kristo.

Philippians 3:8

Kwa kweli

"Kwa uhakika"au Kweli kweli"

Nayahesabu

anaelezea na kuweka msisitizo tangu pale paulo alipo acha kuwa Falisayo na kuwa mfuasi na muumini wa Yesu Kristo

Nayahesabu mambo yote kuwa bure

Paulo anaeleza kuwa ni upuuzi kuweka matumaini katika mambo mengine pasipo Kristo Yesu

kwa sababu ya ubora wa kumjua Kristo Yesu Bwana wangu ni wathamani zaidi"

kwa sababu ya kumjua Kristo Yesu Bwana wangu

Kwa ajili yake nimeacha mambo yote

"Kwa sababu yake ninatarajia kutupa kila kitu mbali"

kuweka mbali

tumia neno lako unalifahamu kwa ajili ya usivyovihitaji milele.

Nayahesabu kama takataka

Paulo anazungumzia vitu ambavyo alivyokuwa anavitumainia lakini baadae anaviona kama takataka na kuvitupa kwenye jalala.

ili nimpate Kristo

"ili nimpate Kristo peke yake"

na niwe ndani yake

Kirai "kupata" ni lugha ambayo inasisitiza wazo la "kuwa" "na kuwa pamoja na Kristo"

Sina haki yangu binafsi kutoka kwenye sheria

"Sijaribu kumpendeza Mungu mimi mwenyewe kwa kutii sheria"

Nguvu ya ufufuo wake

"Ni kufahamu nguvu ya ile itupayo uzima"

ushirika katika mateso yake

ni ile hali ya kushiriki mateso yake

Na nimebadilishwa na Kristo katika mfano wa kifo chake

Neno "badilisha"lina maanisha kugeuza kitu katika hali nyingine kifo cha kimeleta matokeo katika uzima wa milel. Hivyo Paulo anataka kifo chake kifanane na kile cha Yesu,kwamba aweze kuupata uzima wa milele

angalau niweze kuwa na matumaini katika ufufuo wa wafu

Neno "angalau" Paulo hajui nini kinakwenda kutokea katika haya maisha, lakini chochote kitakachotokea, kitakuwa matokeo ya maisha milele. "hivyo basi, haijalishi nini kimetoke sasa, nitaendelea kuishi hata nitakapokufa"

Philippians 3:12

Sentensi unganishi

Paulo anawaagiza waumini wa Filipi kufuata mfano wake kwa sababu ya mbingu na miili mipya iniyowasubiria waamini. Anazungumza vile alivyofanya kwa juhudi ili kuwa kama Krsto, akijua kwamba Mungu atamruhusu aishi mbinguni milele.

Nimeishayapata

Hii inajumuisha katika kumfahamu Krist, kufahamu nguvu za ufufuo wake, mateso yake na kupata kile tunachostahili katika ufufuo na kifo chake Kristo Yesu

au kwamba nimekuwa mkamilifu

"Kwa hiyo mimi sio mkamilifu" au "hivyo mimi sijakomaa bado"

Bali najitahidi

"Bali ninajaribu"

Naweza kupata

"Ninaweza kuyapokea"

kile ninachoweza kukipata katika Krsto Yesu Bwana wetu

"Hii inaweza kuanza na muundo kamili. "kwa sababu ndio maana Yesu ameniita wake"

Ndugu

Tafsiri kutoka 1:12

Nimekwisha kupata mambo haya

"haya mambo yote bado mmiliki wake ni mimi"

Nasahau ya nyuma natazamia ya mbele

Kama mwanaraidha kwenye mstari hashulikii mambo ya kwenye mstari yeye anaangalia yaliyoko mbele yake. "Mimi sijali kile nilichofanya nyuma; mimi ninashughulikia kwa bidii niwezavyo kupata kilichoko mbele yangu"

Najitahidi kufikia lengo kusudi ili niweze kupata tuzo ya juu ya wito wa Mungu katika Kristo Yesu

Kama mwanariadha anakimbia kwenda mbele kwa ajili ya kuvuka mstari. Paulo anakimbia mbele katika kutumika na kuishi katika maisha ya kumtii Kristo.

juu ya wito

Paulo anazungumzia kuishi milele na Mungu kana kwamba Mungu alimwita Paulo na kumtuma.

Philippians 3:15

Sisi tulioukulia wokovu, tunapaswa kuwaza namna hii.

Paulo alitaka wakristo wenzake wawe na hamu ile ile kama yeye alivyo. Kuwa imara katika imani Kufikiri katika jambo moja.

Mungu pia atalifunua hilo kwenu

"Mungu pia atalifanya wazi kwako" au "Mungu atakuhakikishia unalijua"

Mungu atakifunua hilo kwenu

Mungu ataweza wazi hilo jambo au kitu hicho kwako/kwenu

Kwa vyovyote tulivyokwisha kuwa , na tuenende katika hali hiyo

Na tuendelee kuutii ukweli wa neno la Mungu ule ambao tumekwisha pata tayari.

Philippians 3:17

Niigeni mimi

"Fanya yale ninayofanya"au ishi kama ninavyoishi.

ndugu

neno hili humaanisha Wakristo wenza, ikijumuisha wanaume na wanawake, kwa kuwa waumini wote katika Kristo ni washiriki wa familia moja ya kiroho, ambayo Mungu ni baba wa mbinguni.

wale wanaotembea kwa mfano wetu

"wale wanaoishi kama ninavyoishi au wale tayari wanafanya yale niyafanyayo"

wengi wanaishi... kama maadui wa msalaba wa Kristo

Haya maneno ni wazo kuu la Paulo katika mstari huu.

Wengi wanatembea

"Wengi wanaishi"

wale ambao mara nyingi nimewaambieni , na sasa na nawaambia kwa machozi

Paulo anaingilia/anadakia wazo lake kuu kwenye haya maneno ambayo yanaeleza "nyingi."

Nimewaambia mara nyingi

"Nimewaambia mara nyingi"

ninawaambia kwa machozi

"ninawaambia kwa huzuni kubwa"

kama maadui wa msalaba wa Kristo

Hapa "msalaba wa Kristo" inarejea kwa mteso ya Kristo na kifo" Maadui ni wale wasemao wanamwamini Yesu lakini hawako tayari kuteseka au kufa kama Yesu alivyofanya.

Mwisho wao ni uharibifu

"Siku moja Mungu atawaharibu"

miungu wao ni tumbo

Hapa "tumbo" hurejea kwa matamanio ya furaha ionekanayo. Kuita miunga yao inamaana kwamba wanataka heshima ya kuonekana zaidi kulikuwa wanavyotakiwa kumtii Mungu. "wanatamani chakula na heshima nyingine zaidi kuliko kutamani kumtii Mungu"

kiburi chao kipo katika aibu yao

Hapa "aibu" inasimama badala ya matendo ambayo watu wangetakiwa kuonea aibu lakini hawafanyi hivyo. "wanajivunia vitu ambavyo vitawasababishia aibu"

Wakifikiria mambo ya kidunia

Hapa "kidunia" inarejea kila kitu ambacho kitoacho heshima ya kuonekana na hawamheshimu Mungu "Yate wafikiriavyo ni kile kiwapocho heshima wao kuliko kitakacho mpa heshima Mungu"

Philippians 3:20

Maelezo ya jumla:

Kwa matumizi ya Paulo ya "yetu" hapa, amejijumuisha yeye na waamini katika Filipi

Uraia wetu uko mbinguniau

"mji wa nyumbani kwetu ni mbinguni"au nyumbani kwetu halisi ni mbinguni.

Atabadilisha miili yetu

"atabadilisha miili hii minyonge,miili ya asili au tuliyonayo hapa duniani"

kuwa kama mwili wake wa utukufu

"katika miili ifananayo na mwili wake wa utukufu"

mwili, unaowezesha kuvidhibiti vitu vyote kweke

"atabadilisha miili yetu kwa ileile anayotumia kuvitawala vitu vyote"

Philippians 4

Wafilipi 04 Maelezo kwa ujumla

Dhana muhimu katika sura hii

"Furaha yangu na taji langu"

Paulo alikuwa amewasaidia Wafilipi kukomaa kiroho. Kwa sababu hiyo, Paulo alifurahia na Mungu akamheshimu na kazi yake. Aliazimia kufanya wafuasi wa Wakristo wengine na na kuwatia moyo wa kukua kiroho kama ilivyo muhimu katika maisha ya kikristu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#spirit and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#disciple)

Uwezekano mwingine wa utata katika tafsiri ya sura hii

Euodia na Sintike

Ni wazi kwamba hawa wanawake wawili walitofautiana. Paulo aliwasihi waelewane. Walichotofautiana siyo muhimu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

__<< | __

Philippians 4:1

Sentensi unganishi

Paulo anaendelea na baadhi ya maelekezo kwa waamini wa Filipi kuhusu umoja na kuwapa maelekezo kuwasaidia kuishi kwa ajili ya Bwana.

Maelezo ya Jumla

Wakati Paulo anaposema, "watenda kazi wa kweli pamoja," "neno wewe ni umoja. Paulo hasemi jina la mtu. Anamuita hivyo kuonyesha amefanya kazi na Paulo kueneza injili.

Kwa hiyo wapendwa wangu ambao nawatamani

"Waumini wenzangu, nawapenda na ninatamani sana kuwaona"

ndugu

hapa anamaanisha Wakrsto wenza, ikijumuisha wanaume na wanawake, kwa kuwa waumini wote katika Kristo ni washiriki wa familia moja ya kiroho, ambayo Mungu ni baba wa mbinguni.

Furaha na taji yangu

Paulo anatumia neno "Furaha"akimaanisha kuwa kanisa la Filipi nicho kisababishi cha furaha yake. Taji ilitengenezwa kwa majani na mtu aliivaa kichwani kwake kama ishara ya heshima baada ya ushindi alioupata kwenye mchezo. Neno "taji" linamanisha kuwa kanisa la Filipi lilimletea Paulo heshima kwa Mungu. AT:" Mnanipa furaha kwa sababu mmemwamini Yesu, na ninyi ni zawadi na taji

Kwa njia hii simameni imara katika Bwana, enyi rafiki wapendwa

"Kwa hiyo endeleeni kuishi kwa Bwwana katika namna ambayo nimewafundisha, enyi marafiki wapendwa"

Ninamsihi Audia, na ninamsihi Sintike

Hawa ni wanawake waumini waliomsaidia Paulo katika kanias la Filipi. Ninamsihi Audia, na ninamsihi Sintike

Muwe na nia ileile katika Bwana

"Sentensi hii ya "muwe na nia ileile" inamaanisha kuwa na tabia au mawazo yaleyale. "kukubaliana ninyi kwa ninyi kwa kuwa nyote mnamwamini Bwana yuleyule

pamoja nanyi pia

Hapa "wewe" inarejea kwa "mtenda kazi mpendwa" and kama umoja

mtenda kazi

hiki kifungu cha maneno kinatokana na kilimo, ambapo wanyama wawi wangweza kuunganishwa kwenye kongwa/ yoki. "mtenda kazi"

Pamoja na Kelement

Kelement alikuwa Muumin na mtenda kazi katika kanisa laFilipi

Ambao majina yao yamenandikwa kwenye kiabu cha uzima

"Ambao majina yao Mungu ameyaandika kwenye kitabu cha uzima"

Philippians 4:4

Muwe na furaha itokanayo na Bwana siku zote. Tena nasema muwe na furaha

Paulo anawaambia wakristo wa Filipi. Airudia amri ya kufurahi ili kuonyesha msisitizo wa umhimu wa kufurahia. "Furahini kwa sababu ya kile ambacho Bwana amefanya, tena nasema iweni na furaha"

Bwana amekaribia

Sentensi hii imetumika kulenga maana mbili ambazo ni: 1) Bwana Yesu Kristo yuko karibu na wakristo katika roho. 2) Siku ya Bwana Yesu kurudi duniani iko karibu

bali fanyeni mambo yenu yote kwa njia ya kuomba, kusali na kushukuru, mahitaji yenu yajulikane na Mungu

"mwambieni Mungu mahitaji yenu kwa kusali kushukuru"

Iliyo juu ya fahamu zote

"ile iliyozaidi ya uelewa wetu"

italinda mioyo na mawazo mawazo yenu

Hii inawakilisha amani ya Mungu kama askari alindaye hisia zetu na mawazo yetu kutoka kwenye hofu. "itakuwa kama askari na akilinda hisia zako na mawazo kutoka kwenye uoga kuhusu masumbuko ya haya maisha"

Philippians 4:8

Hatimaye

Hili ni hitimisho la sehemu hii ya waraka. Paulo sasa anaelekea kutoa muhtasari wa jinsi wakristo wanavyotakiwa kuishi pale wanapohitaji amani ya Mungu.

ndugu

Neno hili humaanisha Wakristo wenza, ikijumuisha wanaume na wanawake, kwa kuwa waumini wote katika Kristo ni washiriki wa familia moja ya kiroho, ambayo Mungu ni Baba wa mbinguni

kama kuna mambo ya upendo

"ni mambo yanayopendeza"

kama kuna mambo yenye taarifa njema

"haya ni mambo ambayo watu huyatamani" au "mambo ambayo watu huyaheshimu"

kama kuna mambo ya busara

"haya ni mambo ya busara na tabia njema"

na kama kuna mambo yanayohitaji sifa

"kama kuna kisababishi cha sifa"

yale miliyojifunza, mliyopokea, na kuniona nikifanya

'yale niliyowafundish na kuwaonyesha"

Philippians 4:10

Sentensi Unganishi:

Paulo anazungumzia kuhusu waamini wa Filipi wamekuwa wakimsaidia kifedha na kumalizia na salam na shukran.

kuridhika

"kutosheka" au "kufurahi"

katika mazingira yote

"haijalishi mazingira niliyo nayo"

Nafahamu kuishi katika hali ya kupungukiwa...kuwa na vingi

Paulo anajua jinsi ya kuishi maisha ya furaha aidha akiwa hana au akiwa navyo.

namna ya kula wakati wa shibe na jinsi ya kula wakati wa njaa, yaani vingi na kuwa mhitaji

Ki-msingi sentensi hizi mbili zinamaanisha kitu kile kile. Paulo huzitumia kusisitiza kuwa amejifunza kurithika katika mazingira ya namna yeyote ile.

Ninaweza kufanya haya kwa kuwezeshwa na yeye anitiaye nguvu.

"Naweza kufanya mambo yote kwa sababu Kristo hunipa nguvu"

Philippians 4:14

katika dhiki zangu

"wakati ambapo mambo yanakuwa magumu"

mwanzo wa injili

Hii humanisha wakaati Paulo alipokuwa akisafiri kwenda maeneo mbalmbali kwa ajili ya kuwaambia watu habari za Yesu.

hakuna kanisa lililoniwezesha katika mambo yanayohusu utoaji na kupokea isipokuwa ninyi peke yenu.

"ninyi ndiyo kanaisa pekee lililonitumia pese au mlionisaidia"

nasema ili mpate matunda yaletayo faida kwenu

Paulo analinganisha zawadi za kanias na utajiri wa mtu ambao unaongezeka zaidi na zaidi. Paulo anawataka Wafilipi watoe matolea ili wapate baraka za kiroho. "Napenda kumuona Mungu akiwapeni baraka za rohoni zaidi na zaidi"

Philippians 4:18

Nimepokea vitu vyote, na sasa nimejazwa na vitu vingi

Paulo alipokea kila kitu ambacho Wafilipi walimtumia

Nimejazwa

Paulo anamaanisha kujazwa vitu ambavyo yeye mwenyewe.

Ni vitu vizuri vyenye kunukia mithili ya manukato, vyenye kukubalika abavyo vyote ni sadaka inayompendeza Mungu

manukato yenye kunukia, yenye kukubalika inayompendeza Mungu. Paulo anafananisha sadaka za kanisa la Filipi na zile za zilizokuwa zikitolewa kipindi cha Agano la Kale. Makuhani waliteketeza zile sadaka, ambazo zilikuwa zikinukia kwa Mungu. Paulo anasisitiza kwamba sadaka zina thamani kubwa kwa Mungu. "Ninawahakikishieni kuwa sadaka hizi zinampendeza Mungu"

atawajazeni mahitaji yenu

"atatoa kila hitaji mlilonalo"

kwa utajiri wa utukufu wake katika Yesu Kristo

"kutoka kwwenye utajiri wa utukkufu ambao huutoa kupitia Kristo Yesu"

Sasa kwa Mungu

Neno "sasa" limetumika kuonyesha mwisho wa maombi na hitimisho la waraka huu.

Philippians 4:21

Ndugu

anawazungumzia wale watu ambao penginenwalitumika pamoja au na Paulo.

ndugu

neno hili humaanaisha Wakristo wenza, ikijumuisha wanaume na wanawake, kwa kuwa waumini wote katika Kristo ni washiriki warithi wa familia moja ya kiroho, ambayo Mungu ni baba wa mbinguni.

kila muumini...waumini wote

Baadhi ya matoleo yametafsiri kutumia "mtu mtakatifu" na "watu watakatifu"

hususani wale wa familia Kaisari

Hii inazungumzia watumishi waliofanya kazi kwenye eneo la Kaisari.

pamoja na roho zenu

Paulo anazungumzia waumini kwa kutumia neno "roho," ambayo huwawezesha wanadamu kuhusiana na Mungu. "pamoja nanyi"

UTANGULIZI WA WAKOLOSAI

Sehemu ya 1: Utangulizi kwa ujumla

Muhtasari ya kitabo cha Wakolosai

  1. Salamu, kushuhuru na sala (1:1-12)

  2. Yesu na kazi yake

  3. Majaribu ya uaminifu

  4. Mafunzo na maisha

  5. Tabia ya Kikristo (4:2-6)

  6. Kumalizia na salamu

Nani aliandika kitabu cha Wakolosai?

kitabu cha Wakolosai kiliandikwa na Paulo.Paulo alitoka katika mji wa Tarso. Hapo awali alijulkana kama Saulo. Kabla ya kuwa Mkristo, Paulo alikuwa Mfarisayo. Aliwatesa Wakristo. Baada ya kuwa Mkristo, alisafiri mara nyingi katika eneo lote la ufalme wa Warumi akiwahubiria watu kumhusu Yesu.

Paulo aliandika barua hii akiwa jela la Roma.

Kitabu cha Wakolosai kinahusu nini?

Paulo aliandika waraka huu kwa waumini wa Asia Ndogo walioko katika jiji la Kolosai. Lengo kuu la barua hii ni kuittetea injili kutokana na walimu wa uongo. Alifanya hivi kwa kumsifu Yesu kama taswira ya Mungu, anayekidhi vitu vyote na kuwa mkuu wa Kanisa. Paulo alitaka wafahamu kwamba Kristo ndiye alyehitajika ili wakubaliwe na Mungu.

Kichwa cha Kitabu hiki kitafsiriwe namna gani?

Watafsiri wanaweza amua kukiita kitabu hiki na jina lake la asili, "Wakolosai," ama wanaweza kutumia kichwa cha kueleweka zaidi kama "Barua ya Paulo kwa kanisa la Kolosai", ama "Barua kwa Wakristo wa Kolosai." (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-names).

Sehemu ya 2: Maswala muhimu ya kidini na Kitamaduni

Maswala gani ya kidini yalitatanisha kanisa la Kolosai?

Kanisa la Wakolosai lilkuwa na walimu wa uongo. Mafundisho yao kamili hayajulikani. Kuna uwezekano waliwafundisha wafuasi wao kuwaabudu malaika na kufuata sheria kali za sherehe za kidini.Kuna uwezekano mkubwa kwamba walifundisha kwamba lazima wanaume watahiriwe na pia kuepuka aina fulani za chakula. Paulo pia alisema kwamba mafundisho ya uongo pia yalitoka kwa akili ya watu na siyo Mungu.

Paulo alitumiaje istiara ya mbingu na nchi?

Kwenye waraka huu, Paulo amezungumzia mara nyingi mbingu kama iliyo juu akiitofautisha na ardhi inayozungumziwa kama iliyo chini. Lengo la istiara hii ni kufundisha Wakristo waishi kwa njia inayomheshimu Mungu aishie juu mbinguni. Paulo hafundishi kwamba dunia hii iliyeumbwa ina uovu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#evil).

Sehemu ya 3: Maswala muhimu ya Tafsiri

Namuna gani Maswala ya 'takatifu' na 'kutakasa' yamewakilishwa katika Wakolosai ndani ya ULB?

Maandiko yanatumia maneno haya kuashiria baadhi ya maswala mengi. Kwa sababu hii ni vigumu kwa Watafsiri kuyawakilisha vema katika matoleo yao. Katika Wakolosai, maneno haya hutumika kuashiria WaKristo bila kuelezea majukumu yao. Kwa hivyo Wakolosai katika ULB hutumia "Waumini" ama "Walio na imani ndani yake." (Tazama: 1:2,12,26).

Je, Yesu aliumbwa ama alikuwepo tangu mwanzo?

Yesu hakuumbwa lakini amekuwa akiishi kama Mungu.Yesu pia alichukua umbo la binadamu. Kuna uwezekano mkuu wa kutatanisha katika Wakolosai 1:15 inayosema " Yeye ndiye mzaliwa wa kwanza wa viumbe wote."Kauli hii inamaanisha kwamba Yesu ni mkuu kwa vyumbe wote. Haimaanishi kwamba Yesu ndiye kiumbe wa kwanza kuumbwa na Mungu. Watafsiri wawe makini wasimaanishe Yesu ni kiumbe.

Paulo anamaanisha nini na maelezo "ndani ya Kristo,"Ndani ya Bwana," na kadhalika?

Paulo alitaka kueleza juu ya muungano wa karibu sana kati ya Kristo na waumini. Angalia utangulizi wa kitabo cha Waroma kwa maelezo mengine kuhusu maneno haya.

Ni maswala gani muhimu katika maandishi ya kitabu cha Wakolosai?

Matoleo mengine ya kisasa yanatofautina na ya kale kwenye mistari ifuatayo. Toleo la ULB lina maandishi ya kisasa na imeweka maandishi ya kale kama maelezo ya chini ya tanbihi.Iwapo kuna Biblia katika eneo kwa ujumla, watafsiri wanafaa kuamua kutumia maandishi kwenye matoleo hayo. Kama sivyo, watafsiri wanashauriwa kufuata maandishi ya kisasa.

(See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/jit.html#translate-textvariants)

Colossians 1

Wakolosai 01 Maelezo kwa ujumla

Muundo na Mpangilio

Kama barua ya kawaida, Paulo ananza barua yake katika mistari ya 1-2 kwa kumtambulisha Timotheo na kujitambulisha kwa Wakristo wa Kolosai.

Paulo anazungumzia maswala mawili katika sura hii: Kristo ni nani na amefanyia Wakristo nini.

Dhana maalum katika sura hii

Ukweli wa siri

Paulo anaashiria ukweli wa siri katika sura hii. Jukumu la kanisa katika mipango ya Mungu halikujulikana hapo mwanzo. Lakini sasa Mungu amelitambulisha. Moja ya siri hii inahusisha watu wa Mataifa kuwa na nafasi sawa na Wayahudi katika mipango ya Mungu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#reveal).

Mifano muhimu katika sura hii

Picha za maisha ya Kikristo

Paulo anatumia picha nyingi kuelezea maisha ya Kikristo katika sura hii. Anatumia mifano ya "kutembea" na "Kuzaa matunda." (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#fruit

Sehemu zingine zenye utata katika tafsiri ya sura hii

Kitendawili

Kitendawili ni kauli ya ukweli inayaonekana kuelezea kitu kisichowezekana. Mstari wa 24 ni kitandawili: "Sasa ninafurahia katika mateso yangu kwa ajili yenu." Mara nyingi watu hawafurahi wakati wanapoteseka. Lakini katika mistari ya 25-29 Paulo anaelezea ni kwa nini mateso yake ni mazuri. (Wakolosai 1:24)

| >>

Colossians 1:1

Sentensi Unganishi:

Kupitia barua hii ni kutoka kwa Paulo na Timotheo kwa waumini wa Kolosai, baadaye kwenye barua Paulo anaweka bayana kwamba yeye ndiye mwandishi. Huenda alikuwa na Timotheo na kuandika maneno chini Paulo kama mzungumzaji.

Maelezo ya Jumla:

Kupitia hii barua maneno "sisi," "yetu," na "yakwetu" pamoja na Wakolosai vingenevyo yameandikwa tofauti. Neno "ninyi," "yenu," "yakwenu" yanawahusisha waumini Wakolosai na hivyo ni katika wingi vinginevyo yameandikwa tofauti.

Mtume wa Yesu Krist kwa mapenzi ya Mugu

"Aliyechaguliwa na Mungu kuwa mtume wa Yesu Kristo"

Tunatoa...Bwana wetu...sisi mara kwa mara

Haya maneno hayawajumuishi Wakolosai.

Colossians 1:4

Tumeshasikia

Paulo anajiondoa katika wasikilizaji anasemapo "sisi"

Imani yenu katika Kristo Yesu

"Kuamini kwenu katika Kristo Yesu"

kwa sababu ya tarajio la uhakika lililohifadhiwa kwa ajili yenu mbinguni

Ambalo ni matokeo ya uhakika wenu wa tumaini kwa kile Mungu ametunza mbinguni

kuzaa tunda na kuenea

Hapa Paulo anazungumzia kana kwamba kulikuwa mti au mche/mmea ambao ukuapo na kuzalisha chakula.

ulimwenguni kote

Injili inaene na kukua kupitia dunia iliyojulikana.

neema ya Mungu katika kweli

"neema ya Mungu ya kweli"

Colossians 1:7

mpendwa wetu...mwenzetu...kwa niaba yetu

Neno "yetu" na "sisi" sio pamoja na Wakolosai.

injili mliyojifunza kutoka kwa Epafradito, mpendwa wetu mtumishi mwenzetu, ambaye

"injili. Ambayo hasa umejifunza kutoka kwa Epafradito, ambaye in mpendwa mtumishi mwenzetu na ambaye" au "injili. ni sahihi kile Epafra, mtumishi mwenzetu mwenzetu, aliwafundisha. Yeye"

Epafra, tumishi mpendwa wetu, ambaye ni mtumishi mwaminifu wa Kristo kwetu

Hii ina maana kwamba Epafraalikuwa anafanyakazi kwaajili ya Kristo ambayo Paulo mwanyewe angeliifanyakama asingekuwa gerezani.

Epafra

Epafra alikuwa mwanaume aliyehubiri Injili kwa watu wa Kolosi

mpendwa wenu katika Roho

Roho Mtakatifu amewazesha kupenda waumini

Colossians 1:9

Sentensi Unganishi:

Kwa sababu Rohi amewawezesha kuwapenda wengine, Paulo anawaombea na kuwaambia hapa vile aombavyo kwa ajili yao.

Kwa sababu ya upendo huu

"Kwa sababu Roho Mtakatifu amewawezesha kupenda waumini wengine."

Tulisikia...hatujaacha...tumekuwa tukiuliza...tumekuwa tukiomba

Hii inaonyesha Paulo na Timotheo lakini si waumini wakolosai

tangu siku tuliposikia hivi

"tangu siku Epafra alipotuambia haya mambo"

kwamba mtajazwa na maarifa ya mapenzi yake

Paulo anazungumzia waumini wa Kolosai kana kwamba walikuwa chombo cha kubebea. "kwamba Mungu atawajaza kwa kile mnachohitaji kukijua hivyo basi mtafanya mapenzi yake"

Katika hekima yote na ufahamu wa kiroho

"Hekima na ujuzi mmpewa kwa Roho Mtakatifu"

kwamba mtembee katika ustahimilivu wa Bwana katika yeye

"Kwamba muishi katika njia ambayo Ingempendeza Mungu"

katika njia zinazompendeza

"katika njia ambazo zitampendeza Bwana"

Mzae matunda

Hii inalingashwa na mti uzaao matunda kwa kazi nzuri ya waumini.Kama mmea ukuao nakuzaa matunda, hivyo pia waaumini ni kukua katika kumjua Mungu na katika kutenda matendo mema.

Colossians 1:11

Tunawaombea

Neno 'sisi' linaonyesha Paulo naTimotheo lakini si Wakolosai

katika uvumilivu na ustahivu

Paulo anawazungumzia waamini Wakolosai kana kwamba Mungu atawahamishia eneo la uvumilivu. Katika uhalisia, anaomba kwamba hataacha kumwamini Mungu na kwamba watakuwa wavumilivu kikamilifu kadiri waendeleavyo kumhesimu.

aliyewafanya muweze kuwa na sehemu

"amewaruhusu kuwa na sehemu"

mmestahilishwa

Hapa Paulo analenga kwa wasomaji wake kama wapokeaji wa baraka za Mungu.Hamanishi kuwa yeye mwenyewe hana ushirika katikabaraka zile.

Kwa ushirikakatika urithi

Kupokea ambacho Mungu amewaahidi waamini kinazungumziwa kana kwamba kulikuwa na kitu cha kurithi na wanafamilia kurithishwa.

Katika Mwanga

"Kaika utukufu wa uwepo wake"

Colossians 1:13

Sentensi Unganishi:

Paulo anazungumzia kuhusu njia katika Kristo ni nzuri.

Ameokoa

"Mungu Baba amekwisha kuokoa"

katika utawala wa giza

Giza ni picha ya kawaida kwenye maandiko kwa uovu. "nguvu ya uovu"

Mwanae mpendwa

"Mungu ni Baba wa mwana mpendwa, Yesu Kristo"

Katika mwanae tuna ukombozi

mara nyingi Paulo anawaongelea waamini wapi "katika" Yesu Krsto au "katika" Mungu. "Mwanae ametukomboa sisi"

Msamaha wa dhambi

"Mwanae ametusamehe dhambi" au "Baba

Colossians 1:15

Mwana ni mfano wa Mungu asiyeonekana

Kwa kujua kwamba Yesu mwana ni kama, tunaweza kujua Mungu Baba alivyo.

Mwana

hili ni jina muhimu kwa Yesu, Mwana wa Mungu.

Ni mzaliwa wa kwanza

"Mwana n i mzaliwa wa kwanza."Yesu ni muhimu sana na ni wa pekee, "mwana" wa Mungu. Ni Mungu.Neno "Mwana"inaonyesha uhusiano wa ndani na Baba.Uhusiana huu haufahamiki mpaka na vinginevyo uelezwe katika maneno ya lugha kwa 'mwana' na 'baba.'

Kwa sababu ya yeye vitu vyote viliumbwa

"Kwa sababu mwana aliumba vitu vyote"

Hata enzi au mamlaka au utawala vitu vyote viliumbwa na yeye kwa ajili yake

Mwana aliumba vitu vyote kwa ajili yake, kujumlisha kiti cha enzi, utawala, ya kifalme na mamlaka.

Yeye ni mtangulizizwa vitu vyote

"Amekuwepo kabla yavitu vyote"

Katika yeye vitu vyote hushikamanishwa pamoja

"Anashikamanisha kila kitu pamoja"

Colossians 1:18

Yeye ni kichwa

"Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, ni kichwa."

Yeye ni kichwa cha kanisa, yaani mwili wake

Hii inalinganisha nafasi ya Yesu kwa kanisa kama kichwa katika mwili wa kibinadamu.

Mwanzilishi

yeye ni mtawala wa kwanza au mwanzilishi. Yesu alianzisha wa kanisa

Mzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu

Yesu ni mtu wa kwanza kufa na kurudi katika uhai, hatakufa tena.

Mwana

Hii ni jina muhimu sana kwa Yesu, mwana wa Mungu.

Kupitia damu ya mwana ya msalaba wake

asili yaneno "Kupitia" ni wazo la mtiririko au njia, inaonyesha kwamba Mungu huleta amani na upatanisho kwa watu kwa damu ya Yesu alipokufa msalabani.

damu ya msalaba wake

Hapa "damu" inasimama badala kifo cha Kristo msalabani.

Colossians 1:21

Sentensi Unganishi:

Kristo hubadilisha dhambi za waumini wa mataifa kwa utakatifu wake.

Na wewe pia

"Na ninyi Waamini wa Kolosai pia"

Mlikuwa wageni kwa Mungu

"Mlikuwa mmtengwa kutoka kwa Mungu" au "mlikuwa mmesukumwa mbali naMungu."

kuwaleta ninyi watakatifu, wasio na lawama mbele yake

Paulo anawaeleza Wakolosai ingawa Yesu aliwasafisha, kuwaweka katika nguo safi, na kuwaleta kusimama mbele ya Mungu Baba.

bila lawama, na bila dosari

Paulo anatumia maneno mawili yenye maana zinazokaribiana kusisitiza wazo la ukamilifu. "kamili"

mbele yake

"katika mtazamo wa Mungu" au "fikra ya Mungu"

iliyotangazwa

ambayo waumini walitangaza

kwa kila mtu aliyeumbwa chini ya mbingu

"kwa kila mtu katika dunia"

injili ambayo mimi, Paulo, nimekuwa mtumishi

Paulo alikuwa mtumishi wa Mungu halizi. "injili ambayo mimi, Paulo, akimtumikia Mungu kwa kutaingaza"

Colossians 1:24

Natimiliza katika katika mwili wangu kile kinachopungua kwa mateso ya Kristo

Paulo anazungumzia mateso anayoendelea kuyapata. Yawezekana alikuwa anateseka mno ambapo yeye na Wakristo wote lazima wapitie kabla Kristo hajaja tena, na kwamba Krsito hupata pamoja nao kiroho haya magumu.

Natimiliza katika mwili wangu

Paulo anazungumzia mwili wake kana kwamba kilikuwa chombo cha kubebea ambacho kingeweza kubebea mateso.

kwa ajili ya ajili mwili wake , ambao ni kanisa

mara nyingi Paulo anazungumzia kanisa, kundi la waamini wote, kana kwamba ulikuwa mwili wa Kristo.

kulijaza neno la Mungu

Hii inamaana kuleta lengo la ujumba wa injili ya Mungu, ambayo inatakiwa kuhubiriwa na kuaminiwa.

Huu ni ukweli wa siri uliokuwa umejificha

Hii inaweza katika muundo kamili. "huu ni ukweli ambao Mungu alikuwa ameuficha"

kwa miaka mingi na vizazi na kwa miaka

Neno "miaka" na "vizazi" inarejelea kwenye kipindi tangu uumbaji wa dunia mpaka kipindi wakati inijili ilipohibiriwa.

sasa imefunuliwa

"sasa Mungu ameifunua"

utajiri wa utukufu wa siri ya kweli

Paulo anazungumzia thamani hii siri ya ukweli Mungu kana kwamba kulikuwa na hazina ya kupata malighafi. "utajiri"

Kristo yumo ndani yenu

Paulo anawazungumzia waamni kana kwamba walikuwa vyombo vya kubebea ambapo Kristo yupo. Hii ni moja ya njia yake kuelezea umoja wa waamini pamoja Kristo.

Ujasiri wa utukufu ujao

"ambao mnaweza utarajiwao kusemwa kwa utukufu wa Mungu"

Colossians 1:28

tunayemtangaza...tunamwonya...tunamfundisha...tunaweza kumleta

Haya maneno hayawajumuishi Wakolosai.

tunamwonya kila mtu

"Tunamwonya kila mmoja"

Kwamba tumfikishe kwa Mungu kila mmoja

"kwamba tumfikishe kwa Mungu kila mmja"

Kikamilifu

"Wazima Kiroho"

Colossians 2

Wakolosai 02 Maelezo kwa ujumla

Maswala muhimu katika sura hii

Tohara na ubatizo

Katika mistari ya 11-12, Paulo anatumia alama ya tohara ya agano la kale pamoja na alama ya ubatizo ya agano jipya kuchora taswira ya jinsi Wakristo wameungana na Kristo na kuokolewa kutoka kwa dhambi,

ehemu zingine zenye utata katika tafsiri ya sura hii"

Nyama

Hili ni swala ngumu. Labda "nyama" inatumiwa kama mfano ya asili yetu ya dhambi. Paulo hasemi kwamba mwili wa binadamu una dhambi. Ni kama Paulo anajaribu kusema kwamba wakati Wakiristo wanaishi ("katika nyama"), tutaendelea kutenda dhambi. Lakini asili yetu mpya itakuwa inapigana na asili yetu ya kale. Paulo anatumia pia "nyama" katika sura hii kumaanisha mwili wa binadamu.

Maana iliyosemwa

Paulo amevitaja vitu vingi katika sura hii kuashiria mambo yaliyokuwa yanalikumba kanisa la Wakolosai. Ni vyema kuacha maandiko yabaki bila kuelezea kwa uwazi kuhusu maswala yenyewe ya ukweli, (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

<< | >>

Colossians 2:1

Sentensi unganishi:

Paulo anaendelea kuwatia moyo walioamini katika Kolosai na Laodekia wapate kuelewa kuwa Kristo ni Mungu na anaishi ndani ya walioamini ili wapate kuishi sawasawa na walivyompokea.

Ni mapambano ya jinsi gani niliyopitia kwa ajili yenu

Paulo amefanya bidii nyingi katika kuendeleza usafi wao na uelewa wa injili.

Wale waliopo Laodekia

Huu ulikuwa mji karibu sana na Kolosai ambamo pia kulikuwa na kanisa ambalo Paulo alikuwa akiliombea.

kama ambavyo wengi hawajaniona uso wangu katika mwili

"wengi ambao mimi binafsi sijawaona" au "wengi ambao sijaonana nao uso kwa uso"

kwamba mioyo yao

"kwamba mioyo ya wote walioamini ambao hawakuwa wamemuona Paulo"

walioletwa pamoja

waliowekwa pamoja katika ushirika halisi wa karibu

utajiri wote wa uhakika kamili wa maarifa

Paulo nazungumza na mtu anauhakika kamili kwamba habari njema ni kweli ingawa huyo mtu alikuwa tajiri katika mwili huu.

siri ya Mungu ya kweli ya Mungu

Huu ufahamu ambao unaweza kufunuliwa na Mungu peke yake.

ambaye ni, Kristi

Yesu Kristo ndiye siri ya kweli iliyofunuliwa na Mungu.

Katika yeye hazina za hekima na maarifa zilizofichika

Kristo pekee ndiye awezaye kufunua hekima ya kweli ya Mungu na maarifa. "Mungu ameficha hazina zote za hekima na maarifa katika Kristo"

hazina ya hekima na ufahamu

Kimsingi Paulo anazungumzia hekima na maarifa ya Mungu kana kwamba vilikuwa malighafi ya utajiri.

hekima na ujuzi

Kimsingi haya maneno hapa haya maneno yanamaanisha vitu viwili. Paulo ametumia yote pomaja kusisitiza kwamba ufahamu wote wa kiroho unatokana na Kristo.

Colossians 2:4

hila

Hii inamaana kwamba kusababisha mwingine aamini kitu ambacho sio kweli, hivyo, anatenda hiyo imani, na madhara ya mateso kama matokeo.

hotuba yenye ushawishi

hotuba ambayo itafanya mtu afikirie tofauti

sio pamoja nanyi katika nyama

"siko pamoja nanyi kimwili"

Niko nanyi katika roho

"Naendelea kufikiri kuwhusu ninyi"

mpangilio mzuri

kufanya vitu kwa mpangilio

nguvu ya imani yako

"kukosaje na hakuna anayeweza kuwasababishia kuacha kuamini"

Colossians 2:6

mwimarishwe...mjengwe...mjengwe...nyingi

Haya maneno yanaeleza inamaana gani "kutembea katika yeye."

kwamba mlimpokea

"kwamba ninyi waamini wa Kolosai mlimpokea Kristo"

mwimarishewe katika yeye

Paulo anamzungumzia mtu mwenye imani ya kweli katika Kristo kana kwamba huyo mtu alikuwa unaokuwa kwenye aridhi mgumu ngumu yenye mizizi mirefu.

muimarike katika imani

"muishi maisha yenu kulingana na imani yenu katika Yesu Kristo"

kama mlivyofundishwa

Huu ni mwanzo mzuri bila kutaja au vinginevyo kuvuta usikivu kwa mwalimu, ambaye alikuwa Epafradito. "kama mlivyojifunza" au "kama walivyokufundisha" au "kama alivyowafundisha"

muwe na shukurani nyingi

"muwe na shukurani kwa Mungu"

Colossians 2:8

Sentensi unganishi:

Paulo anawasihi walioamini wawe makini wasigeukie maneno na taratibu za wengine kwa sababu hakuna kinachoweza kuongezeka katika ukamilifu wa Mungu walio nao walioamini katika Kristo.

Ona kwamba

"Iweni makini kwamba" au "Angalieni kwamba"

kuwanasa

Paulo anazungumzia vile ambavyo mtu anavyoweza kuamini mafundisho ya uongo (kwa sababu wanaamini mafundisho ya uongo au wanapenda vitu vitu vya uongo)

falsafa

mafundisho ya kidini na imani yasiyotoka katika neno la Mungu lakini yanatokana na mawazo ya ya watu kuhusu Mungu na maisha

maneno matupu ya udanganyifu

haya ni mawazo ya upotoshaji ambayo hayatuongozi katika maisha ndani ya Kristo. Hayazalishi chochote; ni matupu au hayana thamani.

tamaduni za kibinadamu na juu ya mifumo ya dhambi ya dunia

tamaduni zote za Waisraeli na wapagani (watu wa Mataifa) mifumo ya imani haina maana.

kwa kuwa katika yeye ukamilifu wote wa Mungu unaishi kwa jinsi ya mwili

"kwa sababu asili yote ya Mungu inaishi katika mwili wa Kristo"

Colossians 2:10

katika yeye pia mlitahiriwa

Paulo anawazungumzia wale ambao ni wa Kristo kana kwamba walikuwa walikuwa ndani ya mwili Kristo. "wakati ulipojiunga kanisani kwa kubatizwa, God alikubatiza"

mmejazwa katika yeye

Paulo anazungumzia watu ingawa walikuwa chombo cha kubebea kwenye sehemu ambayo Mungu alimuhifadhi Kristo. mmekamilishwa katika Kristo"

Yeye ni kichwa

Kristo ni mtawla

tohara isiyofanywa na wanadamu

katika mfano huu, Paulo anasema kwamba Mungu amewafanya Waamini wa kikristo kukubalika kwa yeye mwenyewe

Mlizikwa pamoja na yeye katika ubatizo

Paulo anazungumzia kuwa na ubatizo na kujiunga na kusanyiko la waamini kana kwamba ilikuwa imezikwa pamoja na Kristo. "Mungu amewazika pamoja na Kristo wakati mlipojiunga na kanisa katika ubatizo"

Katika yeye mlifufuliwa

Kwenye mfano, Paulo anazungumzia maisha mapya ya kiroho ya waamini, walifanywa mitume kwa sababu Mungu alimfanya Kristo kufufuka tena. Hii inaweza kuwa hai. "kwa sababu mmejiunga na wenyewe kwa Kristo, Mungu amewafufua"

Colossians 2:13

wakati mlipokuwa mmekufa

"wakati ninyi waumini wa Kolosai mlikuwa mmekufa kiroho"

mlikuwa mmekufa .... aliwafanya kuwa hai

Fumbo hili linaonesha jinsi gani baada ya kutoka katika maisha ya dhambi kwenda maisha mapya ya kiroho ilivyo kama mtu anayefufuka kutoka kifo.

mmekufa katika hatia zenu na kutokutahiriwa kwa miili yenu

mlikuwa mmekufa katika mambo mawili: 1) mlikuwa mmekufa kiroho, mkiishi maisha ya dhambi dhidi ya Kristo na 2) mlikuwa hamkutahiriwa kulingana na sheria ya Musa.

alitusamehe sisi hatia zetu zote

"Yesu Kristo alitusamehe sisi Wayahudi na ninyi watu wa Mataifa makosa yetu yote"

alifuta kumbukumbu za madeni zilizoandikwa na taratibu zilizokuwa kinyume nasi

Fumbo hili hufananisha jinsi ambavyo Mungu anaweza kuondoa dhambi (deni zetu) na kutusamehe sisi kwa kuvunja sheria za Mungu (taratibu) kama ambavyo mtu anaweza kufuta kitu kilichoandikwa kwenye karatasi.

aliwaongoza katika ushindi na milki

Katika kipindi cha Warumi, ilikuwa kawaida kwa jeshi la Kirumi kuwa na "gwaride la ushindi" waliporudi nyumbani, kuonesha wafungwa wote na mali walizoteka.

kwa msalaba

Hapa "msalaba" unasimama bdala ya kifo cha Kristo msalabani.

Colossians 2:16

katika kula au katika kunywa

Sheria ya Musa ilijumuisha nani anaweza kula au kunywa. "kwa nini mnakula au mnakunywa"

kuhusu siku ya sikukuu au mwezi mpya, au siku za Sabato

Sheria ya Musa ilielekeza siku za kusherehekea, kuabudu, na kutoa sadaka.

kivuli cha vitu vijavyo

"Kivuli" hutoa wazo la mfano wa asili ya kitu halisi. Kwa njia hiyo hiyo, tamaduni za kidini kama vile Sheria za Musa zinaweza kwa kiasi kuonesha uhalisia wa Yesu Kristo.

kiini

Hapa inamaanisha "uhalisia" kitu ambacho kitoacho "kivuli"

Colossians 2:18

mtu yeyote...asidhulumiwe tuzo yake

"mtu yeyote asidanganywe juu ya tuzo yake."

anayetamani unyenyekevu

Neno "unyenyekevu" linasimama badala kwa ajili ya matendo mwingine anawafanya wengine kufikiria kwamba mwingine ni mnyenyekevu. "anayetaka kufanya mambo kuonyesha kwamba wewe ni mnyenyekevu

kuingia kwenye vitu alivyoviona

Hapa Paulo anazungumzia kuhusu watu wanaojiita kuwa na ndoto na maono kutoka kwa Mungu na wanaongea kwa majivuno kuhusu weneyewe.

kushawishiwa na mawazo yake ya kimwili

Hapa Paulo anasema kwamba hali ya kufikiria kaatika hali ya dhambi hufanya mtu awe na kiburi. "anayejiunua kwa maana ya ya mawazo yake ya mwili"

kushawishiwa

Hapa ni mtu anayejivuna anazungumziwa kana kwamba ndani ya chombo ambacho kilichokuwa na hewa kufanya kirefu kuliko kilivyotakiwa kuwa.

mawazo yake ya mwilini

Hii inamaanisha kufikiri kama mtu wa kawaida au mwenye dhambi badala ya kama mtu wa rohoni.

yeye hana shirika na

"Yeye hashikilii kwa nguvu" au "Yeye hatulii katika," kama vile mtoto awategemeavyo wazazi wake

Kristo, aliye kichwa, ambaye katika yeye mwili wote umeunganishwa kwa mishipa na mifupa

Mfano huu hulinganisha mamlaka ya Kristo juu ya kanisa na kichwa cha mwanadamu ambacho kinaongoza na kusimamia mwili wote.

Colossians 2:20

Ikiwa mmekufa pamoja na Kristo katika mtiririko wa imani ya dhambi za ulimwengu.

Fumbo hili linaonesha kwamba, kama vile mtu anavyokufa kimwili hayatii tena mahitaji ya kimwili ya ulimwengu ( pumzi, kula, sleep), mtu anayekufa kiroho pamoja na Kristo haitaji tena kuyatii mambo ya duniani .

Kwa nini mnaishi kama manawajibika kwa dunia: "msiguse"?

Paulo ametumia swali hili, kukemea Wakolosai kwa ajili ya imani isiyo ya kweli ya ulimwengu. Acheni kujinyenyenyekesha kwa imani za ulimwengu.

ishi kama mnawajibika kwa dunia

"fikiri lazima mzitii tamaa za dunia"

dunia

mawazo, tamaa, na dhana za wingi wa dhambi katika dunia ya watu

yameamriwa kwa ajili ya uharibifu

"kuangamia." Paulo hapa anatumia mfano kuchimbua mwili ("uharibifu") kwenye kaburi.

Sheria hizi zinahekima ya dini zilizotengenezwa kwa ubinafsi na unyenyekevu na mateso ya mwili

kutengeneza dini na unyenyekevu na nguvu ya mwili- "Hizi sheria zinaonekana pana kuamini watu kwa sababu zinawaruhusu wale ambao wanaowafwata kuonekana wanyenyekevu kwa sababu wanaumiza miili yao wenyewe"

hazina thamani dhidi ya tamaa za mwili

"msiache kusaidia kufuata mwili wa tamaa"

Colossians 3

Wakolosai 03 Maelezo kwa Ujumla

Muundo na Mpangilio

Sehemu ya pili ya sura hii inafanana na Waefeso 5 na 6.

Maswala muhimu katika sura hii

Nafsi ya kale na nafsi mpya

Nafsi ya kale na nafsi mpya inamaanisha mtu wa kale na mtu mpya. Neno "Mtu wa kale" humaanisha asili ya dhambi ambayo mtu huzaliwa nayo. "Mtu mpya" ni asili mpya ama maisha mapya ambayo Mungu humpa mtu baada ya kuanza kumwamini Kristu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith)

Sehemu zingine zenye utata katika tafsiri ya "sura hii

Tabia

Maswala mengi Paulo anawahimiza wasomaji wake kufuata ama kuacha siyo matendo bali ni tabia. Kwa sababu ya hii, ni ngumu kutafsiri. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-abstractnouns)

"Vitu vilivyo juu"

Makazi ya Mungu mara nyingi huashiriwa kama "juu." Paulo anasema "Tafuta vitu vilivyo juu" na "fikiria kuhusu vitu vilivyo juu." Hapa anamaanisha Wakristo watafute vitu vya umungu na mbinguni.

<< | >>

Colossians 3:1

Sentensi unganishi:

Paulo anawaonya walioamini kwamba kwa kuwa ni wamoja pamoja na Kristo, kuna mambo ambayo waumini hawapaswi kuyafanya

Mungu amewafufua pamoja na Kristo

Kama vile Mungu alivyo mfufua Kristo kutoka kwa wafu, hivyo anawahesabu waumini wa Kolosai kama waliofufuliwa kwenda mbinguni.

mambo yaliyo juu

"mambo ya mbinguni" au "mambo ya kimungu"

kwa kuwa mmekufa

Kama Kristo alivyokufa, hivyo Mungu anawahesabu waumini wa Kolosai kama wamekufa na Kristo.

maisha yenu yamefichwa pamoja na Kristo

Paulo anazungumzia wale watu waishio kana kwamba walikuwa alama ambayo inayoweza kujificha kwenye chombo cha kubebea.

ambaye ni maisha yenu

Kristo ni yule atoaye uzima wa kiroho kwa waamini.

Colossians 3:5

fisheni, mambo yaliyo katika nchi

Paulo anazungumzia tamaa ya dhambi kana kwamba walikuwa sehemu ya kutumia watu kuwashuhudia.

Uchafu

"tabia zisizo safi"

shauku

"kutamani kwa nguvu"

na tamaa, ambayo ni Ibada ya sanamu

"na tamaa, ambayo ni sawa na ibada ya sanamu" au " na msiwe na tamaa kwa sababu ni sawa na kuabudu miungu"

ghadhabu ya Mungu

hasira ya Mungu kinyume na wale ambao hufanya uovu kama kuonyesha kwa kile anafanyacho kuwaadhibu.

wana wasiotii kutotii.

"mwanadamu kutotii" au "watu ambao hawamtii"

"Ni katika mambo haya kwamba ninyi pia hapo kwanza mlitembea kwayo mlipoishi nao."

"Paulo anazungumzia vile ambavyo tabia ya mtu kana kwamba ilikuwa barabara au njia anayotembelea. "Haya ni yale mliyokuwa mkiyafanya"

mlipoishi kati yao

Inaweza kuwa na maana hizi? 1) "unapokuwa umefanyia mazoezi haya mambo" au 2) "unapokuwa umeishi miongoni mwa watu ambao hawamtii Mungu"

ghadhabu, hasira

Neno "hasira" hapa linamaanisha wakati mtu anapokuwa na hasira kwa wale ambao hawamuheshimu kama kuonyesha kwa matendo yake, ambapo italeta madhara kwa watu.

nia mbaya

"tamaa ya kufanya matendo maovu"

hasira

hasira kali sana

matusi

"kururu" au "lugha chafu." Hii inarejea kwa hotuba ambayo inatumika kwa dhamira ya kuumiza wengine

hotuba ichukizayo

maneno ambayo yasioyofaa katika mazungumzo ya upole

kutoka kinywani kwenu

Hapa "kinywa" inasimama badala ya kuzungumza. "katika mazungumzo yenu"

Colossians 3:9

Sentensi unganishi:

Paulo anaendelea kuwaambia waumini jinsi ya kuishi na anawakumbusha kwamba Kristo alifuta kuta ambazo zingekuwepo kati ya Wamataifa na Wayahudi, watumwa na walio huru.

mmeuvua mballi utu wenu wa kale wenyewe pamoja na matendo yake, na mmevaa utu wenu mpya.

Fumbo hili linajenga wakristo ambao wanapaswa kuondoa matendo yasiyo ya kimungu na kuanza kutenda kimungu kwa mtu ambaye anaondoa mavazi machafu na kuvaa mavazi mapya yaliyo safi.

picha yake

Hili linamzungumzia Yesu Kristo

hakuna mgriki au myahudi, kutahiriwa au kutokutahiliwa, msomi, asiye msomi, mtumwa, asiye mtumwa

Hii ni kusema kwamba Mungu anamuona kwa sura ileil, sio kwa jamii, dini, utaifa, au tabaka (hai ya kijamii). " jamii, dini, tamaduni, na hali ya ekijamii

mtu wa Scythia

huyu ni mgeni ambaye hajui mila za mahala pale

asiyesoma

Huyu ni mtu kutoka nchi ya Scythia, ambayo ilikuwa nje ya himaya ya Rumi. Wagiriki na Warumi walitumia hili neno kwa mtu aliyekulia katika sehemu ambayo kila mmoja alifanya mambo maovu mda wote.

Kristo ni vitu vyote, na katika vyote

hakuna kilicho tenganishwa au kuachwa kwenye uwepo wa Kristo. "Kristo ni wa muhimu kwa watu wake wote."

Colossians 3:12

Vaeni...moyo wa huruma

Kama vile mtu awezavyo kuvaa nguo anapokuwa amevaa, waumini wanapaswa kuvaa huruma, unyenyekevu, nk. katika tabia zao kwa kila mmoja.

Kwa hiyo

"Kwa sababu kile nilichokisema ni kweli"

kama wateule wa Mungu - watakatifu na wapendwao

"kama watakatifu wa Mungu na wanaopendwa kwa pendo kuu waliochaguliwa."

ukarimu

"mpole" au "mpole"

unyenyekevu

"unyenekevu wa akili" au "upole wa akili"

upole

"upole"

chukulianeni ninyi kwa ninyi

"fanyeni kazi kwa pamoja katika maelewano na upendo. "chukulianeni na kila mmoja" au " vumilianeni na kila mmoja"

Hurumianeni kwa kila mtu

"Heshimu kila mmoja bora kuliko wanavyostahili kuheshimiwa"

ana lalamiko dhidi

"malalamiko dhidi"

ambao ni dhamana ya ukamilifu

"ambao unatufungamanisha kikamilifu pamoja" au "ambao unatufungamanisha pamoja katika maelewano kamili"

Colossians 3:15

Amani ya Kristo iwaongoze katika mioyo yenu

Paulo anazungumzia amani ambayo Kristo atoayo kana kwamba ilikuwa sheria. inaweza kuwa 1) "fanyeni mabo yote ili kwamba muweza kuwa na mahusiano ya amani kwa hiyo mnaweza kuwa na mahusiano ya amani na kila mmoja" au 2) "Mruhusu Mungu akupe amani kwenye mioyo yenu"

katika mioyo yenu

Neno "Yenu" lina rejea kwa waumini wa Kolosai.

Neno la Kristo likae ndani yenu

Paulo anzungumzia neno la Kristo kama lilikuwa mtu anayeweza kuishi ndani ya mtu mwingine. "siku zote tumaini ahadi za Kristo"

peaneni mawaidha ninyi kwa ninyi

"peaneni tahadhari ninyi kwa ninyi"

ni kwa Zaburi na nyimbo na tenzi za roho

"pamoja na aina zote za nyimbo kumsifu Mungu"

shukurani katika mioyo yenu

"mioyo ya shukurani"

katika maneno na katika matendo

kuongea au kufanya

"katika jina la Bwana Yesu"

"kumwabudu Bwana Yesu" au "pamoja na mamlaka ya Bwana Yesu"

kupitia yeye

"kupitia Bwana Yesu"

Colossians 3:18

Sentensi Unganishi:

Paulo anatoa baadhi ya maelekezo muhimu kwa wake, waume, watoto, kina baba, watumwa, na mabwana.

Wake, nyenyekeeni kwa

"Wake, tiini"

ni sahihi

"ni sahihi" au "ni sawa"

msiwe wakali dhidi ya

"msiwe wakali na" "msiwe na hasira juu ya"

msiwachokoze watoto wenu

"msiwachochee watoto wenu"

Colossians 3:22

tiini mabwana zenu kulingana na mwili

"tiini mabwana zenu wa kidunia"

sio kwa huduma ya machoni kama watu wa kufurahisha

"Vitu. msitii pale tu wakati Bwana wenu anawatazama, kama ambavyo mnatakiwa kuwafurahisha watu"

kama kwa Bwana

"kama muwezavyo kufanya kwa Bwana"

"tuzo ya umilikaji"

"zawadi ya urthi"

urithi

Kupokea kile Mungu alichowaahidi waamini kinazungumziwa kana kwamba kulikuwa na mali na utajiri kutoka wanafamilia.

yeyote atendaye yasiyo haki atapokea huku

"Mungu ataadhibu yeyote afanyaye yasiyohaki"

afanyaye uovu

ambaye atendaye makosa yoyote

hakuna upendeleo

"Mungu humuhukumu kila mmoja kwa kiwango kile kile"

Colossians 4

Wakolosai 04 Maelezo kwa ujumla

Muundo na Mpangilio

Wakolosai 4:1 inaonekana kuambatana na sura ya 3 badala ya 4

Maswala Muhimu kwa sura hii

"Kwa mkono wangu mwenyewe"

Ilikuwa kawaida kwa mwandishi wa kale katika inchi za Mashariki ya Karibu kuzungumza na mtu mwingine anaandika chini yanayozungumzwa. Barua nyingi za Agano jipya ziliandikwa namna hivi.Paulo aliandika mwenyewe salamu za mwisho.

Sehemu zingine zenye utata katika tafsiri ya sura hii

Ukweli wa siri

Paulo anaashiria ukweli wa siri katika sura hii. Jukumu la kanisa katika mipango ya Mungu halikujulikana hapo mwanzo. Lakini sasa Mungu amelitambulisha. Moja ya hii siri inahusisha watu wa Mataifa kuwa na nafasi sawa na Wayahudi katika mipango ya Mungu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#reveal).

__<< | __

Colossians 4:1

Sentensi Unganishi:

Baada ya kuongea na mabwana, Paulo anamalizia maelekezo yake maalumu kwa waamini tofauti tofauti katika kanisa la Kolosai.

haki na adili

Haya maneno ni kama kitu kile kile na yametumika kusisitiza vitu ambavyo ni maadili sahihi.

mnaye bwana wa mbinguni

Mungu anataka mahusiano kati ya bwana wa dunia na mtumwa wake wampende Mungu, bwana wa mbinguni, anawapenda watumwa wake wa duniani pamoja na watumwa wa mabwana wa dunia.

Colossians 4:2

Sentensi unganishi

Paulo anendelea kuwapa maelezo waamini juu ya kuishi na kuongea.

Maelezo kwa jumla:

Hapa neno "sisi" linarejea kwa Paulo na Timotheo ila sio Wakolosai.

Endelea kuwa thabiti katika maombi

"endelea kuomba kwa uaminifu" au "endelea kuomba mara kwa mara"

Mungu afungue njia

"Mungu ataandaa fursa"

siri ya kweli ya Kristo

Hii inarejea injili ya Yesu Kristo, ambayo haikueleweka kabla ya kuja Kristo kuja.

Kwa sababu ya lile neno , mimi nilifungwa.

Kwa kutangaza ujumbe ule wa Yesu Kristo sasa nimefungwa.

omba ili niweze kusema kwa uwazi

"omba niwe na nguvu na uwezo wa kutoa ujumbe wa Yesu Kristo kwa uwazi"

Colossians 4:5

Enenda kwa hekima kwa wale walioko nje

Wazo la kuenenda mara nyingi limetumika kwa ajili kungoza maisha ya mtu. "ishi kama kwamba wale ambao sio waamini wataona kwamba mnahekima"

kuokoa mda

"fanya mambo mazuri mnayoweza kwa mda wako" au "weka mda wako kwa busara"

maneno yenu yawe na neema wakati wote. wakati wote ikolee chumvi

"Mazungumzo yenu wakati wote yawe na neema na ya kuvutia."

lazima mjue jinsi ya kuwajibu

" lazima ujue namna ya kujibu maswali ya kila mmoja kuhusu Yesu Kristo"

Colossians 4:7

Sentensi unganishi:

Paulo anafunga na maelekezo maalumu kuhusu watu flani na kwa salamu pia na kwa kila mwamini.

Maelezo kwa jumla:

Onesmo alikuwa mtumwa wa Filimoni katika Kolosai. Alipoteza pesa kutoka kwa Filimoni na kukimbilia Rumi ambako akawa Mkristo kupitia huduma ya Paulo. Sasa Tikiko na Onesmo ndio wanaleta barua za Paulo Kolosai.

Maelezo kuhusu mimi

"kila kitu kilochokuwa kinatokea kuhusu mimi"

watumwa wenzangu

"watumishi wenzangu." Kupitia Paulo mtu aliyehuru, anajiona kama mtumishi wa Kristo na kumwona Tikiko kama mtumishi mwenzake.

kuhusu sisi

Haya maneno hayawajumuishi Wakolosai.

kuweza kutiwa moyo

Moyo ulikuwa katikati ya hisia nyingi. "kuweza kuwatia moyo"

ndugu yetu mpendwa na mwaminifu

Paulo anamwita Onesmo Mkrito mwenzake na mtumishi wa Kristo.

Watamwita

"Tikiko na Onesmo watasema"

kila kitu kilichotokea hapa

Watawaambia waamini wa Kolosai yote yanayochukua nafasi ambapo Paulo napoishi kwa sasa.

Colossians 4:10

Aristarko

Alikuwa amefungwa pamoja na Paulo huko Efeso wakati Paulo alipoandika barua hii kwa Wakolosai.

kama akifika

"kama Marko akija"

Yesu aliyeitwa Yusto

Huyu mtu alikuwa pia mtenda kazi pamoja na Paulo.

"Hao peke yao ni watu wa tohara ni watenda kazi wenzangu katika ufalme wa Mungu.

"Hawa wanaume watatu ni Wayahudi wakristo tunaofanya kazi pamoja nami ya kumtangaza Mungu kama mfalme kupitia Kristo Yesu"

Hawa peke yao wa tohara

"Hawa wanaume Aristarko, Marko na Yusto pekee ni watu waliotahiriwa.

Colossians 4:12

Maelezo kwa Jumla:

Leodekia na Hierapoli walikwa mjini karibu na Kolosai.

Epafra

Epafra alikuwa mtu aliyehubiri injili kwa watu wa Kolosai.

mmoja wenu

"kutoka mji wenu" au "mwanamji mwenzenu"

mtumwa wa Kristo Yesu

"ni kamati ya wanafunzi wa Kristo Yesu"

wakati wote najitahidi kukuweka katika maombi

"Naomba kwa bidii kwa aljili yako"

uweze kusimama kikamilifu na uhakika

"uweze kukomaa na kuwa jasiri"

Mimi ni shahidi yake, kwamba alifanya kazi ngumu kwa ajili yenu

"Nimefanya uchunguzi kwamba alifanya kazi ngumu sana kwa ajili yenu"

Dema

Ni mtendakazi mwingine pamoja na Paulo.

Colossians 4:15

ndugu

Hapa inamaanisha Wakrsto wenzang, kujumuisha wote wanaume na wanawake.

walioko Leokadia

ni mji ulio karibu sana na Kolosai mahali ambapo kulikuwa na kanisa pia

Nimfa, na kanisa lile lililoko ndani ya nyumba yake

mwanamke aliyeitwa Nimfa alitoa nyumba yake iwe kanisa huko Leokadia. "Nimfa na kundi la waumini walikutana nyumbani kwake"

mwambie Arkipo, iangalie huduma ile uliyopewa katika Bwana, kwamba lazima uitimize"

Paulo anatoa mawaidha kwa Arkipo kwa kazi aliyopewa na Mungu na kwamba Arkipo anawajibishwa na Bwana kwa kuitimiza.

Colossians 4:18

Sentensi Unganishi:

Paulo anafunga barua yake kwa salamu zilizoandikwa kwa mkono yake mwenyewe.

Kumbuka minyororo yangu

Paulo anapozungumzia minyororo anamaanisha alipokuwa gerezani. "Nikumbukeni na kuomba kwa ajili yangu wakati nipo gerezani"

Neema na iwe nanyi

Hapa neno "neema" linasimama badala ya Mungu, ambaye huonyesha neema kwa waamini. "Naomba kwamba Bwana wetu Yesu Kristo aendelee kutoa neema kwenu nyote.

Utangulizi wa Wathesalonike 1

Sehemu 1: Utangulizi wa Jumla

Muhtasari wa kitabu cha Wathesalonike 1

  1. Salamu (1:1)

  2. Sala ya Paulo ya shukrani kwa Wakristo wa Thesalonike (1:2-10).

  3. Huduma wa Paulo Thesalonike (2:1-16).

  4. Paulo anashughulikia ukuaji wao wa kiroho

  5. Paulo anamtuma Timotheo kwa Wathesalonike na Timotheo anaripoti kwa Paulo kuhusu huduma huo.

  6. Mshauri yanayotekelezeka

  7. Baraka za mwisho, shukrani na sala.

Nani aliandika Wathesalonike 1

Paulo aliandika Wathesalonike 1. Hapo awali alijulikana kama Saulo. Alitokea mji wa Tarso. Kabla ya kuwa Mkristo alikuwa Mfarisayo na alikuwa akiwatesa sana Wakristo. Baada ya kuwa Mkristo, alisafiri mara nyingi katika ufalme nzima ya Warumi akiwahubiria watu kumhusu Yesu.

Paulo aliandika barua hii akiwa bado anakaa katika mji wa Korinto. Wasomi wengi wanaamini ya kwamba hii ndiyo ilyokuwa barua ya kwanza ya Paulo miongoni mwa barua alizoziandika nyingi.

Kitabu cha Wathesalonike 1 kinahusu nini?

Paulo aliwaandikia barua hii Waumini katika jiji la Thesalonike. Aliandika barua hii baada ya kulazimishwa na Wayahudi kuondoka jiji hilo. Katika barua hii anasema anachukulia ziara yake jijini humu kama iliyozaa matunda ingawa alilazimishwa kuondoka.

Paulo anajibu kwa habari iliyoletwa na Timoteo kuhusu waumini wa Thesalonike.Waumini wa huko walikuwa wanateswa sana. Paulo aliwahimiza kuendelea kuishi maisha yaliyompendeza Mungu. Pia aliwapa moyo kwa kuwaambia kinachofanyika watu wakufapo kabla ya Kristo kurudi.

Kichwa cha kitabu hiki kitafsiriwe vipi?

Watafsiri wanaweza chagua kichwa cha asili kama "Wathesalonike 1" ama "Wathesalonike wa kwanza". Wanaweza pia kuchagua kichwa cha kueleweka zaidi kama "Barua ya Kwanza ya Paulo kwa Wakristo waThesalonike," ama "Barua ya Kwanza kwa Wakristo wa Thesalonike." Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-names)

Sehemu ya 2: Dhana muhimu za kidini na kitamaduni

Nini maana ya "kuja kwa pili kwa Kristo?"

Paulo ameandika mengi kuhusu ujio wa pili wa Kristo duniani. Kristo atakaporudi atawahukumu watu wote duniani. Atatawala vyumbe vyote na kutakuwa na amani kila mahali.

Nini huwafanyikia wanaokufa kabla ya kurudi kwa Kristo?

Paulo aliweka wazi kwamba wote wanaokufa kabla ya kurudi kwa Kristo watafufuka na kuwa na Yesu.Hawatakuwa wafu milele.Paulo aliandika haya kutia moyo Wathesalonike. Hii ni kwa sababu wengi wao walikuwa na wasiwasi kwamba waliokufa wangeachwa nyuma siku kuu ya kurudi kwa Yesu.

Sehemu ya 3: Maswala muhimu ya tafsiri

Paulo alimaanisha nini na matamshi "ndani ya Kristo" na "ndani ya Bwana?"

Paulo alitaka kuelezea dhana ya Mkristo kuwa karibu na Kristo. Tazama utangulizi katika kitabu cha Warumi kwa maelezo zaidi kuhusu swala hili.

Ni maswala gani muhimu katika maandishi ya kitabu cha Wathesalonike 1?

Katika mistari ifuatayo, matoleo ya kale yanatofoautiana na ya kisasa. Toleo la ULB lina masomo ya kisasa na limeweka ya zamani katika maelezo ya chini. Ikiwa kuna utafsiri wa Bibilia katika eneo jumla, watafsiri wanafaa watumie masomo kwenye tafsiri hizo.Kama siyo hivyo Watafsiri wanaombwa kufuata masomo ya kisasa.

(See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/jit.html#translate-textvariants)

1 Thessalonians 1

1 Wathesalonike 01 Maelezo kwa jumla

Muundo na mpangilio

Mstari wa kwanza unatanguliza barua hii kirasmi. Barua za kale katika Mashariki ya Karibu yalikuwa na utangulizi wa aina hii.

Dhana maalum katika sura hii

Ugumu

Watu wengine waliwatesa sana Wakristo wa Thesalonike. Lakini Wakristo hao waliyachukulia mateso hayo kwa njia nzuri. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

| >>

1 Thessalonians 1:1

Maelezo ya Jumla

Paulo anajitambulisha kama mwandishi wa barua na analisalimu kanisa la Watheselonike.

Paulo, Silivanus na Timotheo kwa kanisa.

Paulo ndiye mwandishi wa barua hii

Neema na amani iwe kwenu

Neno "neema" na "amani" ni maumbo kwa mtu anayeishi na watu kwa ukarimu na amani. "Mungu awe mkarimu kwenu na awape amani"

Amani iwe nanyi.

Neno "Nanyi" linaelezea waumini wa Thesalonike.

1 Thessalonians 1:2

Maelezo ya jumla

Katika hii barua "tu" ya husu Paulo Silvana, na Timotheo, isipo kuwa tu imeelezwa vinginevyo.

Huwa tunamshukuru Mungu.

Tunamshukuru Mungu kila wakati.

Tumekuwa tukiwa taja katika maombi yetu.

" Tunawaombea"

Kazi ya Imani

"Matendo ya Imani" au "Kazi yenu kwa Mungu kwa sababu mnamwamini yeye"

1 Thessalonians 1:4

sentensi unganishi

Paulo anaendelea kutoa shukurani kwa waamini walio Theselonike na ana washukuru kwa imani yao kwa Mungu

Ndugu.

"Waumini"

Tunajuaa.

Neno "sisi" linawaelezea Paulo, Silivanus na Timotheo lakini sio Waumini wa Thesalonike.

si kwa neno tu

si kwa kupitia kuhubiri tu

Ila kwa nguvu za Roho Mtakatifu.

Maana halisi zinaweza kuwa, 1. " Paulo na rafiki zake walihubiri kwa nguvu kwa kuwezesha na Roho Mtakatifu" au " 2. Injili inamatokeo makubwa kwa waaminio kupitia kazi ya Roho Mtakatifu".

Wanaume wa namna gani.

"Kwa namna ambavyo tulijitoa kwenu".

1 Thessalonians 1:6

Mmekuwa mfano wa kuigwa.

Kuiga maana yaake ni kutenda kama au kufataa. " mlituiga sisi".

"kulipokea neno"

"kuyapokea mafundisho" au "kuyakubali mafundisho".

Kwa taabu nyingi.

"katika wakati wa mateso makali" au " katika maudhi mengi".

Akaiya

Hii ilikuwa ni wilaya katika kipindi cha nyuma, na kwa sasa inaitwa Ugiriki.

1 Thessalonians 1:8

Limeenea kote

"Limesambaa pote"

Akaiya

Hii ilikuwa ni walaya katika kipindi cha nyuma, na kwa sasa inaitwa Ugiriki.

Kila mahali.

"Sehemu nyingi na kila Mikoa"

Kwa wao wenyewe.

Paulo anaelezea makanisa ambayo yaliwahi kuwapo katika Mikoa iliyokuwa karibu, waliokuwa wamesikia juu ya Waumini wa Thesalonike.

Wao wenyewe.

Kwa hapa "wenyewe" limetumika kusisitiza wale watu waliokuwa wamesikia juu ya waumini wa Thesalonike.

Namna gani ya mapokezi tuliyokuwa nayo pamoja nanyi.

"Kwa namna ya ukalimu mliyotukaribisha".

Mwanae

Hii ni anwani mhimu ya Yesu inayoeleza mahusiano yake na Mungu.

Aliemuinua.

"Ambaye Mungu alimuinua"

Alietuokoa

Paulo anawahusisha waumini aliokuwa akiwaandikia kwenye neno "sisi"

1 Thessalonians 2

1 Wathesalonike 02 Maelezo kwa ujumla

Dhana muhimu katika sura hii

Shahidi ya Mkristo

Paulo anathamini "Shahidi yake ya Kikristo" kama dhihirisho kwamba injili ni ya ukweli. Paulo anasema kwamba kuwa mtakatifu ama kuishi uungu unashuhudia wasio Wakristo. Paulo anatetea tabia yake ili shahidi wake isiathiriwe. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#testimony and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#godly and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#holy)

Kuishi Kikristo

Sheria ya Musa ilihitaji watu kutoa dhabihu ya wanyama au ya nafaka ndani ya hekalu. Mungu hahitaji dhabihu nyakati hizi. Mungu anahitaji watu waishi kama sadaka.Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lawofmoses)

<< | >>

1 Thessalonians 2:1

sentensi unganishi

Paulo aeleza waamini huduma yao na thawabu.

ninyi wenyewe

neno 'wewe' inahusu wa Wathesalonike wauminio.

ndugu

Hapa hii ina maana Wakristo wenzake, ikiwa pamoja na wanaume na wanawake, kwa sababu waumini wote katika Kristo ni wanachama wa familia moja ya kiroho, na Mungu kama Baba yao wa mbinguni.

ujio wetu

neno 'wetu' inahusu Paul, Silvanusi na Timotheo lakini si waumini wa Wathesalonike.

haikuwa haina maana

ilikuwa na thamani sana

mateso na walikuwa jeuri

Paulo alipigwa na kuweka katika jela la Filipi. 'walikuwa wakinyanyaswa na kutukanwa.

miongoni mwa mgogoro uliyokithiri

"pindi mkutano ukiwa na upinzani mkubwa"

1 Thessalonians 2:3

wala hayatoki kwa Ubaya, wala kwa uchafu, wala kwa udanganyifu

Alikuwa mkweli, safi na mwaminifu

tulivyokubalika na Mungu na kuaminiwa

Paulo alijaribiwa na kithibitishwa mwaminifu na Mungu

tunanena

Paulo azungumza kuhubiri injili

"Mungu, ambaye huipima mioyo yetu

"Mungu, ambaye huchunguza mawazo na matendo yetu"

1 Thessalonians 2:5

maelezo ya jumla

Paulo anawambia Watheselonike waamini kuwa mwenendo wake haukuwa katika maneno ya kujipendekeza, ulafi, au kujitukuza

tumia maneno ya kujipendekeza

"Kuongea na wewe kwa sifa za uongo

wala kama kisingizio cha tamaa

"wala sisi hakutumia maneno kama kisingio cha uchoyo ili wewe utupatie vitu

inaweza kudai upendeleo

inaweza kuwa alifanya wewe kutupatia vitu

1 Thessalonians 2:7

kama mama awezavyo kuwafariji watoto wake mwenyewe.

Kama vile mama mpole anavyowafariji watoto wake, hivyo Paulo, Silvanusi na Timotheo alizungumza kwa upole kwa Wathesalonike

tulikuwa na shauku na wewe

"sisi tulikupenda wewe"

Wewe umekuja kuwa mpenzi mwema kwetu

sisi tunamjali kwa ajili yenu kiundani

Ndugu

Hapa hii ina maana Wakristo wenzake, ikiwa ni pamoja na wanaume na wanawake, kwa sababu wote waaminio katika Kristo ni wanachama wa familia moja ya kiroho na Mungu kama Baba yao wa mbinguni.

Kazi yetu na taabu

Maneno "kazi" na "tabu" kimsingi inamaana moja. Paulo ametumia hayo kusisitiza jinsi gani walifanya kazi ngumu "jinsi walifanya kazi ngumu"

Sisi tulifanya usiku na mchana ili tusiweze kuwa mzigo kwa yeyote kati yenu

"Sisi tulifanya kazi ngumu kufnya maisha yetu wenyewe hivyo haukuwa na haja ya kutusaidia sisi

1 Thessalonians 2:10

Takatifu, haki, na bila lawama

Paulo ametumia maneno matatu ambayo kimsingi ni kitu kimoja na kusisitiza kwamba wao tulipokuwa njia nzuri sana.

Baba na watoto wake mwenyewe

Paulo analinganisha jinsi baba kuwafundisha watoto wake kuishi na jinsi wao kuwahimiza na kuwahamasisha waumini kutembea kwa namna ambayo inamstahili Mungu

sisi kukuhimiza na kukuhamasisha wewe

Maneno "kuwahimiza" na "kukuhamasisha" kimsingia ni kitu kimoja. Paulo anayatumia kusisitiza (passionately) wamewahamasisha Wathesalonike "sisi ni nguvu kukuhamasisha wewe

kwenye ufalme na utukufu wake.

Neno "utukufu" inaelezea neno "Ufalme." "kwa ufalme wake mtukufu".

1 Thessalonians 2:13

maelezo ya jumla

Paulo anaendela kutumia "twa" kumaanisha yeye na anao safiri nao.

Kwa sababu hiyo twamshukuru Mungu kila wakati, kwa

"Sisi tunaendelea kumshukuru Mungu kila wakati kwa sababu"

Mlipokea kama kweli ilivyo neno la Mungu

Wathessalonike waliamini ujumbe wa Paulo aliohubiri kuwa ulikuja kutoka kwa Mungu na sio kutoka kwenye mamlaka ya Paulo mwenyewe

ni hili neno linalo fanya kazi kwenu mnao amini

Paulo anazungumzia injili kana kwamba ni mtu anaye fanya kazi

1 Thessalonians 2:14

ndugu

Hapa hii inamaanisha Wakristo wenzetu

mlikuwa wafuasi wa makanisa

Wao wanauzoefu sawa wa uadui kutoka baadhi yaWathessalonike kama vile waamini wa kwanza wazoefu wa mateso kutoka kwa viongozi wa Wayahudi "Ikawa kama makanisa"

kutoka kwa watu wa Taifa lenu wenyewe

"kutoka kwa Wathessalonike

Nao walituzuia sisi tusiseme

"Wao walijaribu kutufanya kuacha kusema"

daima walitimiza dhambi zao

"kuendelea kutenda dhambi"

Ghadhabu imewawajia kwao

"Adhabu ya Mungu imewajia ndani yao" au"'hasira ya Mungu imewajia ndani yao'

1 Thessalonians 2:17

ndugu

Hapa hii inamaanisha Wakristo wenzetu

katika uso, si kwa moyo

"Kimwili lakini sisi tunaendelea kuomba kwa ajiri yenu"

kuona uso wako

"Kukuona wewe" au "kuwa na wewe"

Mimi Paulo mara moja na tena

"Mimi Paulo, alijalibu mara mbili"

Kwa nini ni matumaini yetu ... wakati wa kuja kwake?

"Kujiamin kwetu kwa baadae, furaha, na taji ya utukufu ni wewe na wengine wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu.'

1 Thessalonians 3

1 Wathesalonike 03 Maelezo kwa ujumla

Dhana muhimu katika sura hii

Kusimama

Katika sura hii Paulo anatumia "simama imara" kuonyesha kuwa imara. Hii ni njia ya kawaida ya kuelezea kuwa imara ama mwaminifu. Paulo anatumia "Kutingizwa" kama kinyume cha kuwa imara. Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faithful)

<< | >>

1 Thessalonians 3:1

sentensi unganishi

Paulo anawambia waamini amemtuma Timotheo kuimarisha imani zao.

Hatukuweza kuvumilia.

Neno "sisi" linawaelezea Paulo, Silivanus na Timotheo lakini sio waumini wa Thesalonike. au " hatukuweza kuwa na uvumilivu tukihofu juu yenu"

Ilikuwa vyema kubaki kule Atheni peke yake.

"Ilikuwa vyema kwangu na Silivanus kubaki Atheni.

Vyema

"Vizuri" au "yenye mantiki"

Atheni

Huu ni Mji katika jimbo la Akaiya, ambapo kwa sasa huitwa Ugiriki.

Ndugu yetu.

"Mkristo mwenzetu"

Hakuna ambaye atasumbuliwa

"Hakuna atakayekuwa na matatizo" au hakuna atakaye ondolewa"

Tumeteuliwa.

"Tumekusudiwa"

1 Thessalonians 3:4

Ukweli dhabiti.

"bila shaka" au " uhakika"

Tulikuwa na wewe

Neno "sisi" linawaelezea Paulo, Silivanus naTimotheo lakini sio waumini wa thesalonike.

Kupata mateso.

"kutendewa mabaya na wengine"

Sikuweza kuvumilia.

Kwa hapa " mimi" inamuelezea Paulo: nilitaka kujua.

Nilimtuma.

"Nilimtuma Timotheo"

Bure.

" Isiyofaa"

1 Thessalonians 3:6

sentensi unganishi

Paulo anawambia wasomaji kuhusu taarifa ya Timotheo baada ya kutoka kuwasalimu

Alikuja kwetu

Neno " kwetu" linawaelezea Paulo na Silivanus lakini sio waumini wa thesalonike.

Habari njema ya Imani yako

" Taarifa nzuri juu ya Imani yako"

Mmekuwa na kumbukumbu nzuri

"Mmekuwa na kumbukumbu nzuri mara kwa mara"

Mnatamani kutuona sisi

"Mnashauku ya kutuona sisi"

Ndugu

" kwa hapa " ndugu inamaanisha wakristo wenzao.

Kupitia Imani yenu.

"kupitia imani yenu katika kristo" au "kupitia maendeleo yenu katika kristo"

1 Thessalonians 3:8

kwa sasa tunaishi.

Neno " sisi" linawaelezea Paulo, Silivanus na Timotheo lakini sio waumini wa thesalonike.

Msimame imara.

"Mnaamini kwa sana"

Ni shukurani zipi tumrudishie Mungu kwa ajili yenu, kwa furaha yote tulinayo juu yenu kwa Mungu wetu?

Swali hili rhetorical huonyesha shukrani. AT 'Hatuwezi kumshukuru Mungu ya kutosha kwa ajili matendo yake kwa ajili yako! Sisi sana kufurahi juu yako wakati sisi kuomba kwa Mungu wetu!

Kwa shukrani tunaweza kutoa kwa Mungu kwa ajili yenu, kwa furaha ile yote kwamba tuna mbele ya Mungu juu yako?

Swali hili rhetorical huonyesha shukrani. AT 'Hatuwezi kumshukuru Mungu ya kutosha kwa ajili matendo yake kwa ajili yako! Sisi sana kufurahi juu yako wakati sisi kuomba kwa Mungu wetu!

Usiku na Mchana.

"Mara kwa mara"

Ni ngumu

Bidii

Kuuona uso wako.

"Kukutembelea"

1 Thessalonians 3:11

maelezo ya jumla

katika hii mistari, neno "wetu" halielezei watu wa aina moja kila wakati.

Na Mungu wetu

"Tunaomba ya kuwa Mungu wetu"

Na Mungu wetu...Bwana wetu Yesu.

Neno "wetu' linaelezea waumini wote.

Baba mwenyewe.

"mwenyewe" inamuelezea "Baba" kwa msisitizo.

Zielekeze njia zetu kwako

Neno "zetu" linawaelezea Paulo, Silivanus na Timotheo lakini sio waumini wa Thesalonike.

Pia sisi tunafanya

Neno "sisi" linawaelezea Paulo, Silivanusi na Timotheo lakini sio waumini wa Thesalonike.

Na afanye hivyo

"Tunaomba ya kuwa Mungu atatenda"

Katika ujio wa Bwana wetu Yesu

" wakati Yesu atakapokuja tena duniani"

Na utakatifu wake wote

"Na wale wote waliowakwake"

1 Thessalonians 4

1 Wathesalonike 04 Maelezo kwa ujumla

Dhana muhimu katika sura hii

Uzinzi

Mila mbalimbali zina vipimo tofauti vya uzinzi na kwa hivyo itakuwa vigumu kutafsiri fungu hili.Watafsiri pia ni lazima wafahamu miiko ya kitamaduni. Maneno haya ni maneno yasiofaa kwa adabu sahihi.

Kufa kabla ya kurudi kwa Kristo

Katika kanisa la mwanzo, watu walijiuliza chenye kingefanyika iwapo mtu angekufa kabla ya kurudi kwake Yesu Kristo. Kuna uwezekano kwamba walikuwa na wasiwasi kama waliokufa kabla ya kurudi kwake Kristo wangejumuishwa kwenye ufalme wake. Paulo anajibu swali hilo.

"Kunyakuliwa mawinguni tumlaki Bwana hewani"

Kifungu hiki kinaashiria wakati Yesu atakapowaita wale waliomwamini. Wasomi wanatofautiana iwapo hii inaashiria kurudi kwake Yesu kwa mara ya mwisho kwa utukufu ama hapana. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#believe)

<< | >>

1 Thessalonians 4:1

Ndugu

hapa "ndugu" inamaanisha mkristo mwenzako

Tunawatia moyo na kuwasihi

Neno "sisi" linawaelezea Paulo, Silvanus na Timothy lakini sio waamini wa Thesalonike. Neno "kutia moyo" na "kusihi" inamaana moja. Paulo aliyatumia ili kusisitiza ni kwa jinsi gani wanawatia moyo waamini.

Mlipokea maelekezo toka

"mlifundishwa na"

Lazima mtembee

Hapa neno "kutembea" inaelezea namna ambavyo mtu anatakiwa kuishi.

1 Thessalonians 4:3

Epuka tamaa za mwili

"kaa mbali na tamaa za mwili"

Namna ya kumiliki

"kujua namna ya kuishi na"

Tamaa za mwili

"tamaa mbaya za mwili"

Asiwepo mtu

"asowepo yeyote" au "asiwepo mtu"

Atakayevuka mpaka na kumkosea

Hii ni maelezo zaidi inayoelezea wazo lile lile kwa namna mbili.

Bwana ndiye mwenye kulipa kisasi

"Bwana atamuadhibu yule atakayevuka mipaka na atamtetea yule atakayekosewa"

Tulivyowaonya na kuwashuhudia

"Tulivyowaambia kabla ba kuwaonya kwa nguvu"

1 Thessalonians 4:7

Mungu hakutuita kwa uchafu bali kwa utakatifu

Mungu alituita kuwa wasafi na watakatifu.

Mungu hakutuita sisi

Neno "sisi" linamaanisha waamini wote.

Yeye anayelikataa hili

"Yeyote asiyezingatia mafundisho haya" au "yeyote anayeyapuuzia mafundisho haya"

1 Thessalonians 4:9

Upendo wa ndugu

"upendo kwa waamini wenzako"

Mlifanya yote kwa ndugu walioko Makedonia yote.

"mlionesha upendo kwa waamini wa Makedonia"

Ndugu

Hapa "ndugu" inamaanisha Mkristo mwenzako

Mtamani

"Kujiingiza" au "kujitahidi kwa bidii"

Fanya shughuli zako

Hii inamaanisha usiingilie mambo ya watu wengine.

Fanya kazi kwa mikono yako

"mfanye kazi zenu wenyewe ili mpate kile mnachookiitaji"

Tembea kwa usahihi

"Ishi kwa heshima na tabia njema"

Wale walioko nje ya imani

"wale ambao sio waamini wa Kristo"

Usihitaji kitu chochote

"Usipungukiwe na hitaji lolote"

1 Thessalonians 4:13

Maelezo ya jumla

Paulo anaongelea waamini walio kufa, walio hai, na ao watakao ishi Kristo akirudi.

Hatutaki msielewe.

"Tunataka muelewe"

Hatutaki

"Sisi" inawaelezea Paulo, Silvanus na Timotheo lakini sio waamini wa Thesalonike.

Ndugu

Hapa "ndugu" inamaanisha Mkristo mwenzako.

Kulala

Hapa inamaanisha "kufa."

Msiomboleze

"Msisikitike"

Kama hao wasiojua mambo yajayo

"Kama watu wasioamini"

Kama tukiamini

Hapa "sisi" linawaelezea Paulo na hadhira yake.

Kufufuka tena

"kufufuka na kuishi tena"

Atawaleta pamoja na Yesu hao waliolala mauti.

"akirudi atawafufua waamini waliokufa wakimwamini Yesu"

Kwa ajili ya hayo twasema

"Sisi" linawaelezea Paulo, Silvanus na Timotheo lakini sio waamini wa Thesalonike.

Hakika hatutawatangulia

"hakika hatutakwenda mbele yao"

1 Thessalonians 4:16

Bwana mwenyewe atashuka.

"Bwana mwenyewe atakuja chini"

Malaika mkuu

Malaika mkuu

Waliokufa katika Kristo watafufuka kwanza

Hapa anamaanisha kifo cha kimwili. "wale waliomwamini Yesu Kristo lakini walikufa watafufuka kwanza"

Sisi tulio hai

Hapa "sisi" linamaanisha waamini wote.

Pamoja nao

Neno "wao" linawaelezea waamini waliokufa.

Tutaungana hewani ili kumlaki Bwana mawinguni.

Kumlaki Bwana Yesu

1 Thessalonians 5

1 Wathesalonike 05 Maelezo kwa ujumla

Muundo na Mpangilio

Paulo anamalizia barua yake kama barua za kawaida nyakati za kale kule Mashariki Ya Karibu.

Dhana Muhimu katika sura hii

Siku ya bwana

Wakati kamili wa ujio wa siku ya Bwana itakuwa ni kwa ghafla pasipotarajiwa. Hii ndiyo maana ya "kama mwizi usiku". Kwa sababu hii, Wakristo waishi wakijiandaaa kurudi kwa Bwana. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#dayofthelord and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-simile)

"Kukata kiu ya Kiroho"

Hii ina maana ya kutojali ama kufanya kinyume na mwongozo na kazi ya Roho Mtakatifu.

__<< | __

1 Thessalonians 5:1

sentensi unganishi

Paulo anazidi kuongelea siku Yesu ata rudi

muda na nyakati

"muda ambayo Bwana Yesu atarudu tena "

Ndugu

Her "ndugu" inamaanisha Wakiristo wengine

mwajua ya kuwa

"kufahamu kabisa" au "kuwa na ufahamu"

kama mwizi ajapo usiku

kama vile ambavyo mtu hajui ni usiku gani mwivi atakuja kuvunja na kuiba, sisi hatujui siku ya Bwana itakuja lini. "bilakutazamia"

Pale wasemapo

"Watu watakaposema"

ndipo uharibifu

"ndipo uharibifu usiotegemewa"

kama utungu umjiavyo mama mwenye mimba.

Kama vile mwanamke mjamzito maumivu ya kujifungua mtoto huja ghafla na wala haichi mpaka kuzaliwa itakapokamilika, ndivyo uharibifu huja na watu hawataweza kuepuka.

1 Thessalonians 5:4

ninyi, ndugu hampo kwenye giza

Hapa "ndugu" inamaanisha Wakristo wenzake. "Ninyi si wa dunia hii ya uovu, ambayo ni kama kuwa katika giza"

hata ile siku iwajie kama mwizi

Siku ambayo Bwana atakuja haitakuwa ya kushitukisha kama vile mwizi anavyo mshitukisha mtu. "Isiwapate pasipo kujiandaa"

ninyi nyote ni wana wa mchana...siyo wana wa usiku

Hapa "wana wa mchana" inamaanisha wafuasi wa Kiristo. "wana wa usiku" inamaanisha wale wote wengine wanaofuata dunia.

tusilale kama wengine wafanyavyo

Paulo anafananisha kulala na ile hali ya kutokujua kuwa Yesu atarudi kuhukumu ulimwengu. " tusiwe kama wengine ambao hawajui kuwa Yesu anarudi tena"

tusilale

neno "tu"inarejea kwa waumii wote .

bali tuendelee kukesha na kuwa na kiasi

Walioamini katika Kristo wanatakiwa wawe katika hali ya tahadhari kwa kurudi kwake na kuwa na kuweza kujizuia,

Kwa kuwa wale walalao hufanya hivyo usiku

Kama ilivyo usiku wakati watu wamelala na hawajui nini kinachotokea, ndivyo itakavyokuwa kwa dunia, ambao hawajui kuwa Kiristo atarudi.

wale wanao lewa hulewausiku

Paulo anataja kuwa ni usiku ambapo watu huwa wanalewa, hivyo kama watu hawana ufahamu kuwa Kiristo anarudi hawataishi maisha ya kujizuia

1 Thessalonians 5:8

maelezo ya jumla

katika mistari ya 8-10 "sisi" ya husu waamini wote

wana wa mchana

Hii inawakilisha waumini katika Kristo. "waumini katika Kristo" au "watu wa mwanga."

tuwe na kiasi

"tujizoeze katika kujizuia"

kuvaa dirii ya

kama askari anavyo vaa dree kuulinda mwili wake, Mkiristo aliyeamini anayeishi kwa imani na upendo atapata ulinzi. "tujilinde wenyewe kwa"

kofia ya chuma

kama kofia ya chuma inavyo mlinda askari kichwani, hivyo ndivyo uhakika wa waokovu inavyomlinda muumini. "na ujue"

kwamba tumacho au tumelala

"kwamba tuko hai au tumekufa"

kujengana ninyi kwa ninyi

"kufarijiana"

1 Thessalonians 5:12

Ndugu,

Hapa "Ndugu" humaanisha walioamini wenzake

tuwatambue wale wanaotumika

"Kuheshimu na kuthamini wale ambao wanashiriki katika kuongoza"

na wale wanaowaongoza katika Bwana

Hii inamaanisha wale watu ambao Mungu amewaweka kutumika kama viongozi katika vikundi vya waumini sehemu mbalimbali.

muwatambue na kuwapa heshima kwa upendo kwa sababu ya kazi yao

"Waheshimuni na kuwatii kwa kazi yao kwasababu mnawapenda wao"

1 Thessalonians 5:15

Furahini siku sote, Ombeni bila ukomo, Mshukuruni Mungu kwa kila jambo

Paulo anawatia moyo waumini kuendeleza tabia ya kiroho ya kufurahi kwa kila jambo, kuwa na juhudi katika maombi, na kutoa shukurani kwa mambo yote.

kila jambo

katika hali zote

Kwa kuwa haya ni mapenzi ya Mungu

Paulo anaeleza zile tabia alizo zitaja kuwa ni mapenzi ya Mungu kwa waamini wote.

1 Thessalonians 5:19

Msimzimishe Roho

"Msimzuie Roho Mtakatifu kufanya kazi ndani yenu"

Msiudharau unabii

"Msiwe na dharau kwa unabii" au "Msichukie chochote ambacho Roho Mtakatifu atamueleza mtu"

Jaribuni kila Jambo

"Kakikisha kuwa kila unabii ni kweli na unatoka kwa Mungu"

shikilia lililo jema

Paulo anazungumza ujumbe za Roho Mtakatifu kama ni vitu ambavyo mtu anaweza shika mikononi mwake.

1 Thessalonians 5:23

kuatenga kwa ajili yake kabisa

"awatenge" au "kufanya ninyi msiwe na kosa, hivyo kwamba msitende dhambi"

roho, nafsi na miili wote

Hii ni mfanano ambao neno "roho", "nafsi" na "mwili" kuwa na maana sawa lakini hutumiwa hapa kwa msisitizo.

itunzwe pasipo mawaa katika

"itunzwe isifanye dhambi mpaka"

Yeye aliyewaita ni mwaminifu

"Yeye ni Mwaminifu aliyewaita "

ndiye ambaye pia kutenda.

""atawasaidia ninyi"

1 Thessalonians 5:25

maelezo ya jumla

Paulo anatoa kauli zake za kufunga

ndugu

Hapa "ndugu" ya maanisha wa Kristo

nawasihi katika Bwana

"nawauliza, kama ni Bwana anazungumza nanyi"

barua hii isomwe

hii yawezwa tajwa katika kauli tendaji, "ninyi nyote msome hii barua"

Utangulizi wa 2 Wathesalonike

Sehemu 1: Utangulizi wa jumla

Muhtasari wa kitabu cha 2 Wathesalonike

  1. Salamu na kushukuru (1:1-3)

  2. WaKristo wanaoumia kwa mateso

  3. Kutoelewa kwa waumini wengine kuhusu kuja kwa Kristo kwa mara ya pili

  4. Imani ya Paulo kwamba Mungu atawaokoa Wakristo Wathesalonike

  5. Paulo anatoa ombi la kuombewa na waumini Wathesalonike (3:1-5)

  6. Paulo anatoa amri kuhusu waumini wasiofanya kazi (3:6-15)

  7. Kumalizia (3:16-17)

Nani aliandika 2 Wathesalonike?

Paulo aliandika Wathesalonike 2. Hapo awali alijulikana kama Saulo. Alitokea mji wa Tarso. Kabla ya kuwa Mkristo alikuwa Mfarisayo na alikuwa akiwatesa sana Wakristo. Baada ya kuwa Mkristo, alisafiri mara nyingi katika ufalme nzima ya Warumi akiwahubiria watu kumhusu Yesu.

Paulo aliandika barua hii akiwa anaishi katika mji wa Korintho.

Kitabu cha 2 Wathesalonike kinahusu nini?

Paulo aliandika barua hii kwa waumini katika mji wa Thesalonike. Aliwatia moyo waumini hawa kwa sababu walikuwa wanateswa.Aliwaambia kuendelea kuishi kwa njia inayompendeza Mungu. Alitaka kuwafundisha tena kuhusu kurudi kwa Kristo.

Kichwa cha Kitabu hiki kinastahili kutafsiriwa namna gani?

Watafsiri wanaweza amuru kukiita kitabu hiki kutumia kichwa chake cha kitamaduni, "2 Wathesalonike" ama " Wathesalonike wa pili." ama wanaweza chagua kichwa kinachoeleweka zaidi kama, "Barua ya pili kwa kanisa la Thesalonike," ama "Barua ya pili kwa Wakristo wa Thesalonike," (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-names)

Sehemu 2: Dhana muhimu za kidini na kitamaduni

Nini maana ya "ujio wa pili wa Yesu"?

Paulo aliandika maswala mengi katika barui hii kuhusu kurudi kwake Yesu Kristo duniani.Yesu akirudi, atawahukumu wanadamu wote. Pia atahukumu viumbe wote. Atasababisha kuwepo kwa amani duniani. Paulo pia alieleza kwamba "mwanaume mhalifu" atakuja kabla ya kurudi kwa Kristo.Mtu huyu atamtii Shetani na kufanya watu wengi kumuasi Mungu.Lakini Yesu atamuangamizi huyu mtu atakaporudi.

Sehemu 3: Maswala muhimu ya tafsiri

Paulo alimaanisha na maelezo "ndani ya Bwana," na "ndani ya Kristo,' na kadhalika?

Paulo alitaka kuasilisha swala la muungano wa karibu kati ya Kristo na waumini. Tazama utangulizi wa kitabu cha Warumi kwa maelezo zaidi kuhusu aina hii ya maelezo.

Ni maswala gani makuu ya maandishi ya kitabu cha 2 Wathesalonike?

Katika mistari ifuatayo, matoleo ya kisasa yanatofautiana na matoleo ya kale.ULB ina masomo ya kisasa na huyaweka masomo ya awali kama maelezo ya chini.Iwapo kuna tafsiri ya Bibilia katika eneo jumla, watafsiri wazingatie kutumia masomo yanayopatikana katika hayo matoleo. Kama sivyo, watafsiri wanashauriwa kufuata masomo ya kisasa.

(See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/jit.html#translate-textvariants)

2 Thessalonians 1

2 Wathesalonike 01 Maelezo kwa jumla

Muundo na mpangilio

Mistari 1-2 huanzisha kirasmi barua hii. Barua za kale katika Mashariki ya Karibu zilikuwa na utangulizi wa aina hii.

Maswala mengine ya utata katika tafsiri ya sura hii

Kitendawili

Kitendawili ni kauli ya ukweli ambayo inaonekana kufafanua kitu kisichoezekana. Kitendawili untaokea katika mistari 4-5: "Tunazungumzia uvumilivu wenu na imani yenu katika mateso yenu yote.Tunazungumzia mateso mnayostahimili.Hii ni ishara ya hukumu ya kweli ya Mungu." Watu kila mara hawangefikiria kwamba kumuamini Mungu wakati wa kuteswa ni ishara ya hukumu ya kweli ya Mungu.Lakini katika mistari ya 5-10, Paulo anaelezea jinsi Mungu atawapatia tuzo wale ambao wanamwamini na jinsi atakavyuwahukumu wanaowatesa. (2 Wathesalonike 1:4-5)

2 Thessalonians 1:1

Maelezo ya Jumla:

Paulo ndiye mwandishi wa barua hii, lakini anawajumuisha Silwano na Timotheo kama wapelekwaji wa barua. Anaanza kwa kusalimia kanisa la Thesalonike.

Maelezo ya Jumla:

Maneno "sisi" linamaanisha Paulo, Silwano naTimotheo, au kama limetumika vinginevyo. Pia neno " ninyi" ni wingi na lina maanisha waumini wa kanisa la Wathesalonike.

Silwano

Huu ni muundo wa Kilatini "Silas." Ni mtu yule yule aliyeorodheshwa katika kitabu cha Matendo kama msafiri mwenzi wa Paulo.

Neema iwe juu yenu

Paulo kawaida anatumia salamu hii katika barua zake.

2 Thessalonians 1:3

Maelezo ya Jumla:

Paulo anatoa shukrani kwa ajili ya waumini katika kanisa la Thesalonike.

kupaswa kutoa shukrani kwa Mungu

Paulo anasema anapaswa kumshukuru Mungu mara kwa mara.

ndugu

Hapa "ndugu" inamaanisha Wakristo wenzetu, ikijumuisha wanaume kwa wanawake.

Hivi ndivyo ipasavyo

"kwa kuwa hiki ni kitu sahihi cha kufanya" au " ni vyema"

Upendo ambao kwa kila mmoja amefungamanishwa na mwenzake

"mnapendana nyinyi kwa nyinyi"

kila mtu na mwenzake

Kila mtu na mwenzake lina maanisha Wakristo wenzetu."

sisi wenyewe

Hapa "wenyewe" limetumika kusisitiza kujisifu kwa Paulo.

kwamba mpate kuhesabiwa kuwa mnastahili kwa ajili ya ufalme wa Mungu.

Hii inakwemwa katika muundo tendaji. AT: "kwamba Mungu atawahesu kuwa wa sehemu ya ufalme wa Mungu."

2 Thessalonians 1:6

Sentensi Unganishi:

Paulo anapoendelea, anaoongea kuhusu Mungu kuwa mwenye haki.

ni haki kwa Mungu

"Mungu yuko sahihi" au "Mungu ni wa haki"

na raha kwenu

Unaweza kuifafanua kwamba Mungu ndiye arudishae raha. AT:" na kwamba Mungu arudishe raha kwenu."

malaika wa nguvu zake

"Malaika wa Mungu wenye nguvu"

Katika mwali wa moto atalipiza kisasi kwa wale wasiomjua Mungu na wale

"Bwana Yesu atawaadhibu kwa mwali wa moto wale wasiomjua Mungu na wale" au "Kisha kwa mwali wa moto atawaadhibu wale wote wasiomjua Mungu na wote ambao hawamtii Bwana Yesu" (UDB)

2 Thessalonians 1:9

watateseka

Neno "wataseka" wanamaanishwa watu wasioitii injili.

atakapokuja sike ile

Hapa "siku ile" ni siku Yesu atakaporudi duniani.

ili atukuzwe na watakatifu wake

Hii inaweza kusemwa katika hali halisi. AT: "watu wake waliomwamini watamtukuza "

watastaajabishwa na wale wote walioamini

Hii inaweza kuwa katika hali tendaji. "wale wote walioamini watashangaa" au "wale wote walioamini watamshangaa yeye"

2 Thessalonians 1:11

Pia tunaendelea kuomba kwa ajili yenu

Paulo anasisitiza jinsi anavyoomba mara nyingi kwa ajili yao. AT: Pia mara kwa mara tunaomba kwa ajili yenu.

kuita

Neno "kuita" lina maanisha Mungu anateua au anachagua watu kuwa watoto wake, kuwa watumishi wake na wahubiri wa ujumbe wa wokovu kwa njia ya Yesu.

kutimiza kila haja ya wema

"awawezeshe kufanya mema kwa kila namna mnavyo tamani" (UDB)

ili kwamba mpate kulitukuza jina la Bwana wetu Yesu

Hili linaweza kuelelezewa katika muundo tendaji. AT: "ili kwamba mweze kulitukuza jina la Bwana wetu Yesu"

Ili mtukuzwa na yeye

Hili linaweza kusemwa katika muundo tendaji. AT: "Yesu atawatukuza ninyi"

kwa sababu ya neema ya Mungu wetu

kwa sababu ya neema ya Mungu"

2 Thessalonians 2

2 Wathesalonike 02 Maelezo kwa jumla

Dhana muhimu katika sura hii

"Kukusanyika pamoja "ili tukae naye"

Kifungu hiki kinaashiria wakati ambapo Yesu anawaita wale wanaomwamini. Wasomi wanatofautiana iwapo hii inaashiria kurudi kwa Yesu kwa mwisho kwa utukufu ama kama si hivyo.(Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#believe)

Mtu muasi

Hii ni sawa na "mwana wa uharibifu" na "yule muasi" katika sura hii.Paulo anamhusisha na Shetani ambaye anafanya kazi kwa bidii duniani. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#antichrist)

Anakaa ndani ya hekalu la Mungu

Huenda Paulo anarejelea hekalu la Yerusalemu ambalo liliharibiwa na Warumi miaka chache baada ya kuandika hii barua. Ama anarejelea kwa hekalu lijalo la ukweli, ama kanisa kama hekalu la kiroho la Mungu.(Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

<< | >>

2 Thessalonians 2:1

Maelezo ya Jumla:

Paulo anawaasa waumini wasidanganywe kuhusu siku ambayo Yesu atarudi.

Sasa

Neno "Sasa" linaonyesha kubadilika kwa mada katika maelekezo ya Paulo.

Ndugu

Neno "ndugu" linamaanisha Wakristo wenzetu, linajumuisha wote wanaume na wanawake. AT: " kaka na dada"

Kwamba msisumbuliwe au kuhangaishwa kwa urahisi

kwamba msiruhusu mambo yawasumbue kwa urahisi.

kwa ujumbe au barua ambayo inadhaniwa kutoka kwetu

"kwa maneno au barua iliyoandikwa ambayo inadhaniwa kutoka kwetu.

kwa tokeo kwmba

"kusema kwamba'

siku ya Bwana

Hii inamaanisha wakati atakaporudi duniani kwa ajili ya waumini.

2 Thessalonians 2:3

Maelezo ya Jumla:

Paulo anafundisha kuhusu mtu wa uasi.

haitakuja

"siku ya Bwana haitakuja"

anguko

hii inamaanisha wakati ujao ambao watu wengi watampa Mungu kisogo.

na mwana wa uasi amefuniuliwa

Hii inaweza kusemwa katika muundo tendaji. AT: na Mungu anamfunua mtu wa uasi

mwana wa uaharibifu

Paulo anaongea uharibifu kama mtu alizaa mwana ambaye lengo lake ni kuharibu kila kitu. AT: "yeye aharibuye kila kitu anachoweza"

vyote vinavyoitwa Mungu au vivavyoabudiwa

Hii inaweza kusemwa katika muundo tendaji. AT: "kila kitu ambacho watu hukifanya kuwa Mungu au kila kitu ambacho watu huabudu"

anajiinua mwenyewe kama Mungu

"anajionyesha mwenyewe kama Mungu"

2 Thessalonians 2:5

Hamuyakumbuki...mambo haya?

Paulo anatumiwa swali lisilohitaji kujibiwa kuwakumbusha mafundisho ambayo aliwafundisha awali alipokuwa nao. Hii inaweza kuelezewa kama. AT: " Ninauahakika kuwa mnakumbuka... haya mambo."

mambo haya

Hii ina maanisha kurudi kwa Yesu, siku ya Bwana , na mtu wa kuasi.

atafunuliwa tu kwa wakati muafaka

Hii inaweza kusemwa katika muundo tendaji. AT: "Mungu atamfunua mtu wa uasi kwa muafaka"

siri ya kuasi

Hii ina maanisha kwa siri ambayo Mungu mwenyewe anaifahamu.

anayemzuia

kumzuia mtu ni kuwashikilia nyuma au hali kutowafanya kuendelea na kile wanachotaka kufanya.

2 Thessalonians 2:8

ndipo mwenye kuasi atakapofunuliwa

Hii inaweza kusemwa katika muundo tendaji. AT: Halafu Mungu atamruhusu mwenye kuasi ili kujionyesha mwenyewe.

kwa pumzi ya kinywa chake

Hapa neno "pumzi" linamaanisha nguvu ya Mungu. AT: "kwa nguvu ya neno lake lilotamkwa"

Ufunuo wa kuja kwake utamfanya kuwa sio chochote

Wakati Yesu atakaporudi duniani na kujionyesha, atamshinda yule mwenye kuasi.

kwa nguvu zote, ishara, na maajabu ya uongo

"kwa nguvu zote, ishara, na maajabu ya uongo"

na uongo wote wenye udharimu

Mtu huyu ataumia kila aina ya ubaya kuwadanganyawatu ili wamwamini yeye badala ya Mungu.

Mambo haya yatakuwepo kwa wale wanaopotea

Huyu mtu atapewa nguvu na shetani na atadanganya kila mtu ambaye hakuamini katika Yesu.

wanaopotea

Hapa "potea" lina wazo la milele au uangamivu wa milele

2 Thessalonians 2:11

Kwa sababu hii

" Kwa sababu watu hawapendi kweli"

Mungu anawatumia kazi yenye uongo ili waamini uongo

Paulo anaongea kuwa Mungu anaruhusu kitu kutokea kwa watu kana kwamba anawatumia. AT: "Mungu anaruhusu mtu wa kuasi awadanganye"

wote watahukumiwa

Hii inaaweza kusemwa katika muundo tendaji. AT:" Mungu atawahukumu wote"

wale ambao hawakuamini kweli badala yake wakajifurahisha katika udhalimu

"wale ambao walifurahia udhalimu kwa sababu hawakuiamini kweli"

2 Thessalonians 2:13

Sentence Unganishi

Paulo sasa anabadilisha mada.

Maelezo ya Ujumla:

Paulo anatoa shukrani kwa Mungu kwa ajili ya wakristo na anawatia moyo.

Lakini

Paulo anatumia neno hili hapa kuanzisha kubadili mada.

inatupasa kumshukuru Mungu wakati wote

Hii ni hali ya kukuza tukio au jambo la kawaida na kulifanya kuwa kubwa zaidi kuliko uhalisia wake. AT: "tunapaswa kuendelea kutoa shukrani"

tunapaswa

Neno tunapaswa linamaanisha Paulo, Silwano, na Timotheo.

ndugu mpendwao na Bwana

Hili linaweza kulezwa katika muundo tendaji. AT: "kwa kuwa ndugu Bwana anawapenda"

ndugu

Hapa "ndugu" linamaanisha wakristo wenzangu, inajuisha wanaume na wanawake. AT: "ndugu wa kiume na wakike.

malimbuko kwa ajili ya wokovu

"kuwa miongoni mwa watu wa kwanza kuamini katika Yesu na kuokolewa.

katika utakaso wa Roho

"na kuwatenga ninyi kwa ajili ajili yake kwa njia ya Roho"

imani katika kweli

"kuamini katika kweli" au "kuwa na ujasiri katika kweli"

kwa hiyo, ndugu, simameni imara

Paulo anawaasa waumini waendelee kushikilia imani yao katika Yesu.

elewa tamaduni

hapa "tamaduni" linamanisha kwa ukweli wa Kristo ambao Paulo na mitume walifundisha. Paulo anaongea nao kana kwamba wasomaji wake wangeweza kushika neno kwa mikono yao.

uliyofundishwa

Hii inaweza kusemwa katika muundo tendaji. AT: tuliyowafundisha"

iwe kwa neno au kwa barua yetu

unaeza kuelezea kwa timilifu zaidi habari. AT: "iwe kwa kile tulichowafundisha gerezani au kile tulichowandikieni kwa barua"

2 Thessalonians 2:16

Sentensi Unganishi:

Paulo anamaliza na baraka kutoka kwa Mungu.

Sasa

Paulo anatumia neno hili kuonyesha badiliko la mada.

Bwana wetu ...aliyetupenda na kutupatia

Neno hili "aliyetupenda" na "sisi" linajumisha waumini wote.

Bwana Yesu Kristo mwenyewe

Neno "yeye mwenyewe" liongeza msisitizo kwa neno "Bwana Yesu Kristo."

awafariji na kuifanya imaramioyo yenu

"mioyo" linamaanisha kwenye sehemu ya hisia. AT: "awafariji na kuwaimarisheni kwa"

2 Thessalonians 3

2 Wathesalonike 03 Maelezo kwa jumla

Dhana muhimu katika sura hii

watu wasiofanya kazi na wavivu

atika mji wa Thesalonike, inaonekana kulikuwa na shida ya watu katika kanisa ambao walikuwa na uwezo wa kufanya kazi lakini wakakataa kufanya hivyo. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

Utafanya nini ndugu yako akitenda dhambi?

Katika sura hii Paulo anawafundisha Wakristo kwamba wanastahili kuishi kwa njia inayomheshimu Mungu. Wakristo pia wanastahili kuhimizana na kuajibikiana wanachotenda.Kanisa pia lina wajibu wa kuwahimiza waumini kutubu wakati wanatenda dhambi. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#repent and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

__<< | __

2 Thessalonians 3:1

Maelezo ya Jumla:

Paulo anawaomba waumini waombe kwa ajili yake na wenzake

Na sasa

Paulo anatumia neno "sasa" kubadilisha mada.

ndugu

hapa neno "ndugu" linamaanisha wakristo wenzetu, linajumisha wanaume na wanawake. AT: "ndugu wa kiume na wakike"

neno la Bwana liweze kuenea na kutukuzwa

Paulo anaongea kutawanya kana kwamba Neno la Mungu linakimbia toka sehemu moja kwenda sehemu nyingine. AT: "kwamba watu wengi zaidi na zaidi hivi karibuni watasikia ujumbe wetu kuhusu Bwana wetu Yesu na kuuheshimu"

kwamba tuweze kuokolea

Hili linaweza kusemwa katika muundo tendaji: AT: "kwamba Mungu atuokoe" au " kwamba Mungu aweze kutuokoa sisi"

Kwa sababu sio wote wanayo imani

"kwa kuwa watu wengi hawaamini katika Yesu"

ambaye atawaimarisha ninhyi

"ambaye atawaimarisha ninyi"

yule mwovu

"Shetani"

2 Thessalonians 3:4

Tunao ujasiri

' Tunayo imani" au "tunaamini"

kuongoza mioyo yenu

Paulo anamwelezea Bwana kuwahamasishaWakristo wampende Mungu kana kwamba Bwana alikuwa akiwaongoza katika njia

mioyo

Hii ni sitiari kwa ajili ya hisia au takwa, ambayo inaongoza upendo na uaminifu.

kwa upendo wa Mungu na kwa uvumilivu wa Kristo

paulo anaongea upendo wa Mungu na uvumilivu wa Mungu na Kristo kana kwamba kulikuwa na mwisho katika njia. AT:Ni namna gani gani Mungu anawapenda na jinsi gani ambayo Kristo alivyovumilia kwa ajili yetu.

2 Thessalonians 3:6

Maelezo ya Jumla:

Paulo anawapa waumini maelekezo ya mwisho kuhusu kufanya kazi na sio kukaa bila kufanya kazi.

Sasa

Paulo anatumia neno hili kuonyesha kubadili mada.

katika jina la Bwana Yesu Kristo

"kwa mamlaka ya Yesu"

ndugu

hapa "ndugu" linamaanisha wakristo wenzetu, inajumuisha wote wanaume na wanawake. AT: "ndugu wa kiume na wakike"

Bwana wetu

Neno "wetu" linamaanisha waumini wote.

kuishi bila kufanya kazi

"ni mzembe na anazuia kufanya kazi"

kutuiga sisi

" kufanya kama Paulona wenzake" au " kutenda kama Paulo na watenda kazi wenzake'

Hatukuishi kati yenu kama wale wasio na nidhamu

Paulo anatumia maneno hasi ili kusisitiza maneno chanya. AT: "Tuiishi miongoni mwenu kama waliokuwa na nidhamu sana"

tulifanya kazi usiku na mchana

"tulifanya kazi wakati wa usiku na wakati wa mchana" au "tulifanya kazi muda wote"

katika kazi ngumu na shida

Paulo anasisitizajinsi hali yake ilivyokuwa ngumu. kazi ngumu inamaanisha kazi ambayo inahitaji juhudi kubwa. Ugumu inamaanisha walivumia maumivuna mateso.AT: "katika hali ngumu.

Tulifanya hivi sio kwa sababu hatukuwa ma mamlaka

Paulo anatumia neno hasi kusisitiza upande chanya. Hii inaweza kusemwa kama chanya. AT: "pasina shaka tulikuwa na mamlaka."

2 Thessalonians 3:10

baadhi wanaenenda paipo utaratibu

Hapa "enenda" linasimama kwa kumaanishatabia katika maisha. AT: "baadhi wanaishi maisha ya "kubweteka" au "wengine ni wavivu"

lakini badala yake ni watu wanaoenenda pasipo utaratibu.

Hawa nia watu wanaoingilia mambo ya wengine pasipo kuombwa kufanya hivyo.

kwa utulivu

"katika utulivu, amani utulivu." Paulo anawaasa watu wazembe waiotaka kufanya kazi waache kuchunguza mambo ya wenzao."

2 Thessalonians 3:13

Lakini

Paulo anatumia neno hili kutofautisha kati ya wakristo wavivu na wachapakazi.

ninyi, ndugu

Neno "niny" linamaanisha wakristo wote wa Thesalonike.

ndugu

Neno "ndugu" hapa linamaanisha wakristo wenzangu, inajumuisha wanaume na wanawake. AT: "ndugu wa kiume na wakike"

msizimie roho

"Kuzimia moyo" ni neno linalomaanisha kuchoka, au kukata tama." "msikate tamaa au "msichoke"

muwe makini naye

Mmtambue kuwa ni nani.AT: "mmtambue mbele za watu"

ili kwamba aweze kuaibika

Paulo anawaelekeza waumini kujihadhari nawaumini wavivu kama kitendo cha kuwaadibisha.

2 Thessalonians 3:16

Maelezo ya Jumla:

Paulo anahitimisha maoni/ ufafanuzi wake wakristo wa Thesalonike.

Bwana wa amani mwenyewe awape ninyi

Unaweza kuweka wazi kuwa haya ni maombi ya Paulo kwa Wathesalonike. AT: "Ninaomba kwamba Bwana wa amani mwenyewe awapeni..."

Bwana wa amani mwenyewe

"Mwenyewe" inaelezea kwamba Bwana mwenyewe atawapa amani wakristo.

Hii ni salamu yangu mwenyewe, Paulo, kwa mikono yangu mwenyewe

"Mimi, Paulo, naandika salamu kwa mkono wangu mwenyewe"

Hivi ndivyo niandikavyo

Paul anaweka wazi kwamba hii barua inatoka kwake na sio ya kubumba

Utangulizi wa 1 Timotheo

Sehemu ya 1 Utangulizi kwa ujumla

Muhtasari wa kitabu cha 1 Timotheo

  1. Salamu (1:1,2)

  2. Paulo na Timotheo

  3. Sala kwa wote (2:1-8)

  4. Wajibu na majukumu kanisani (2:9-6:2)

  5. Maonyo

  6. Maelezo kuhusu mtu wa Mungu (6:11-16)

  7. Maelezo kwa Matajiri (6:17-19)

  8. Maneno yakufunga kwa Timotheo (6:20-21)

Nani aliandika kitabu cha 1 Timotheo?

Paulo alikiandika kitabu cha 1 Timotheo. Hapo awali alijulikana kama Saulo. Alitokea mji wa Tarso. Kabla ya kuwa Mkristo alikuwa Mfarisayo na alikuwa akiwatesa sana Wakristo. Baada ya kuwa Mkristo, alisafiri mara nyingi katika himaya nzima ya Warumi akiwahubiria watu kumhusu Yesu.

Kitabo hiki ni barua ya kwanza ya Paulo kwa Timotheo. Timotheo alikuwa mwanafunzi wake na rafiki wake wa karibu. Kuna uwezekano kama Paulo aliandika barua hii akikaribia kufa.

Kitabu cha 1 Timotheo kinahusu nini?

Paulo alikuwa amemwacha Timotheo katika jiji la Efeso kuwasaidia waumini wa huko. Paulo aliandika barua hii kumshauri Timotheo kuhusu maswala mengi. Kati ya maswala aliyoangazia ni swala la kuabudu katika kanisa, na masherti ya waongozi wa kanisa na maonyo kuhusu walimu wa wongo. Barua hii inaonyesha namuna Paulo alifundisha Timotheo kuwa mwongozi wa makanisa.

Kichwa cha kitabu hiki kitafsiriwe namna gani?

Watafsiri wanaweza amua kukiita kitabu hiki kutumia jina lake la kiasili, "1 Timotheo" ama "Timotheo wa Kwanza" ama wanaezatumia kichwa kinachoeleweka zaidi kama "Barua ya Kwanza kwa Timotheo" (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-names)

Sehemu ya 2: Dhana muhimu za kidini na kitamaduni

Uanafunzi ni nini?

Uanafunzi ni hali ya kuwafanya watu wawe wanafunzi wa Kristo. Lengo kuu la uanafunzi ni kuwafanya Wakristo kuwa kama Kristo. Barua hii inatoa mwelekeo jinsi kiongozi anatakiwa kumfunza Mkristo ambaye hajakomaa. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#disciple)

Sehemu ya 3: Maswala muhimu ya tafsiri

Wingi na umoja wa "wewe"

Neno "mimi" katika kitabu hiki linaashiria Paulo. "Wewe" inamaanisha Timotheo. Tofauti ya haya ni 6:21 (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-exclusive and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-you)

Paulo alimaanisha nini na maelezo "ndani ya Kristo" na "ndani ya Bwana" na kadhalika?

Paulo alitaka kuelezea wazo la kuwa na ushirika wa karibu sana kati ya muumini na Kristo. Tafadhali tazama utangulizi wa kitabu cha Warumi kwa maelezo zaidi kuhusu kauli hii.

Ni maswala gani kuu ya kimaandishi katika kitabu cha 1 Timotheo?

Katika aya ifuatayo,matoleo ya kisasa yanatofautiana na matoleo ya kale. Toleo la ULB lina masomo ya kisasa na imeweka masomo ya zamani kwenye tiniwayo(maelezo ya chini). Iwapo tafsiri ya Bibilia inapatikana eneo kwa ujumla, watafsiri wanashauriwa kuzingatia matumizi ya masomo yaliyoko katika matoleo hayo. Kama sivyo, watafsiri wanashauriwa kutumia masomo ya kisasa.

(See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/jit.html#translate-textvariants)

1 Timothy 1

I Timotheo 01 Maelezo kwa jumla

Dhana kuu katika sura hii

Watoto wa Kiroho

Katika sura hii, Paulo anamwita Timotheo "Mwanawe wa Kiume" na "mwanawe"..Paulo alimfanya Timotheo kuwa Mkristo na kiongozi wa kanisa. Kuna uwezekano Paulo pia alimwongoza kumwamini Kristo. Kwa maana hiyo Paulo akamwita Timotheo "mwanangu katika Kristo".

Orodha ya ukoo

Orodha ya ukoo ni orodha ya rekodi ya mababu na wazawa wa mtu. Wayahudi walitumia orodha ya ukoo kuwachagua watu kuwa wafalme. Walifanya hivi kwa sababu ni mtoto tu wa kiume wa mfalme ambaye alistahili kuwa mfalme.Walionyesha pia kabila na familia familia yao. Kwa mfano makuhani walitoka kwa ukoo wa Walawi na wana wa Aruni. Maarufu wengi walikuwa na rekodi za ukoo yao.

Mifano muhimu ya usemi katika sura hii

Maneno yanayohusu jambo moja

Kauli "Sheria ni nzuri mtu akiitumia kisheria" ni maneno yanayoashiria kitu kimoja. Maneno "sheria" na "kisheria" yana usemi sawa katika lugha ya awali.

| >>

1 Timothy 1:1

Maelezo ya jumla

Katika kitabu hiki, neno "Yetu" linamaanisha Paulo na Timotheo.

Paulo

"Mimi, Paulo, nimeandika barua hii." Lugha yako inaweza kuwa na njia tofauti ya kumtambulisha mwandishi wa barua. Tumia njia iliyo sahihi kwenu.

kulingana na amri ya

"kwa amri ya" au "kwa mamlaka ya"

Mungu Mwokozi wetu

"Mungu ambaye alituokoa sisi"

Kristo Yesu tumaini letu

Hapa neno "tumaini letu" humaanisha mtu ambaye tunaweka tumaini letu kwake. "Kristo Yesu, ambaye ni tumaini letu" au "Kristo Yesu katika yeye tunaweka ujasiri wetu"

mtoto wa kweli katika imani

Paulo anaongea juu ya uhusiano wa karibu kati ya Timotheo na Paulo kama ule wa baba na mtoto. Paulo anamchukulia Timotheo kuwa ni mtoto wake kwa kuwa alimfundisha kuwa na imani katika Kristo. Mfano wa tafasiri: "ambaye ni sawa na mtoto kabisa kwangu"

Neema, rehema, na amani

"Basi neema, rehema, na amani iwe kwenu," au "Basi ninyi mpate wema, rehema, na amani"

Mungu Baba

"Mungu, ambaye ni Baba yetu" ni jina la muhimu la Mungu.

Kristo Yesu Bwana wetu

"Kristo Yesu, ambaye ni Bwana wetu"

1 Timothy 1:3

Kauli Unganishi

Paulo anamtia moyo Timotheo kukataa matumizi mabaya ya sheria na atumie vizuri mafundisho kutoka kwa Mungu.

Kama nilivyokusihi wewe

"Kama nilivyokuhimiza wewe," au "Kama nilivyokuomba kwa bidii"

kaeni Efeso

"nisubirini mimi hapo katika mji wa Efeso"

mapokeo mengine

mafundisho mengine tofauti na yale tuliyofundisha sisi.

wala hawatasikiliza kwa makini

"Pia nataka ninyi muwaamuru wasisikilize kwa makini"

hadithi

zinaweza kuwa ni hadithi kuhusu mababu zao.

vizazi visivyo na mwisho

Paulo anatumia "isiyo na mwisho" kusisitiza kwamba vizazi ni vingi.

Hizi husababisha malumbano

"Hizi huwafanya watu kutokubaliana." Watu walijadili kuhusu hadithi na nasaba ambamo hakuna angeweza kujua ukweli wake.

badala ya kusaidia mpango wa Mungu, ambao ni kwa imani

Maana: 1) badala ya kutusaidia sisi kujua mpango wa Mungu wa kutuokoa, ambao tunajifunza kwa imani 2) badala ya kutusaidia sisi kufanya kazi ya Mungu, ambayo tunaifanya kwa imani

1 Timothy 1:5

sasa

Neno limetumika hapa kuonesha kituo kwenye mafundisho ya msingi. Hapa Paulo anaeleza lengo la kile anachomwamuru Tithotheo.

amri

Hii haimaanishi Agano la Kale au Amri Kumi lakini zaidi ni wajibu uliotolewa na Paulo kwenye 1:3.

ni pendo

Inawezekana kumaanisha 1) upendo kwa Mungu au 2) kuwapenda watu.

kutoka moyo safi

Hapa "safi" inamaanisha kuwa mtu hana nia ovu ya kufanya mabaya. Na "moyo" hapa inamaanisha akili na mawazo ya mtu.

dhamiri nzuri

"dhamiri ambayo imechagua haki juu ya mabaya"

imani thabiti

"uaminifu" au "ukweli" au "isiyo na unafiki"

baadhi ya watu wamekosea

Paulo anaongelea imani ndani ya Kristo kuwa shabaha yetu.

na wameasi vitu hivi

"kuasi" kama ilivyotumika hapa ni msemo unaomaanisha kuwa watu wameacha kufanya maagizo ya Mungu.

walimu wa sheria

Hii inamaanisha "sheria za Musa"

Lakini hawaelewi

"ingawa hawaelewi" au "lakini hawaelewi"

1 Timothy 1:9

Na tunajua hiki

"Hiyo ni, sisi tunaelewa hiki" au "Kwasababu tunatambua hili" au "Sisi pia tunajua hili"

haikutengenezwa kwaajili ya mtu mwenye haki

"haikutolewa kwa mtu mwenye haki" au "haikuwekwa kwa mtu anaye tii" au "hakupewa mtu ambaye ni mwenye haki mbele za Mungu"

kwaajili ya wale wauao baba na mama zao

"wauaji wa baba zao na mama zao" au "wale ambao huwaumiza kimwili baba na mama zao"

watu wasio na maadili kingono

Huu ni mfumo wa neno la kiume kwaajili ya malaya wa kike. Kwenye maeneo mengine ilitumika kama sitiari kwa watu wasiowaaminifu kwa Mungu, lakini katika suala hili maana inaonekana kuhusisha mtu yeyote ambaye analala na mtu mwingine nje ya ndoa.

mashoga

"wanaume ambao wanalala na wanaume wengine."

wale ambao wanateka watu kwaajili ya utumwa

"wale ambao wanateka watu kuwauza kama watumwa" au "wale ambao wanachukua watu kuwauza kama watumwa"

injili ya utukufu wa Mungu wa baraka

"injili ya kuhusu utukufu ambao ni mali ya Mungu wa baraka" au "injili ya utukufu na Mungu mbarikiwa"

ambayo nimeaminiwa

"ambayo Mungu amenipa mimi na akanifanya kuwajibika kwayo"

1 Timothy 1:12

Kauli Unganishi:

Paulo anazungumza jinsi alivyotenda zamani na anamtia moyo Timotheo kumtumaini Mungu.

Nashukuru

"Ninashukuru" au "mimi nashukuru kwa"

yeye aliniona mimi mwaminifu

"yeye alinitazama mimi mwaminifu" au "alifikiria kuwa ninafaa"

na akaniweka katika huduma

"na kuniweka katika nafasi ya kutumika" au "hivyo aliniteua katika huduma"

mimi, mtukana Mungu wa zamani

"mimi, ambaye alisema maovu kinyume na Kristo" au "mimi, ambaye nilikuwa mtukana Mungu hapo zamani"

mtu wa vurugu

"mtu ambaye anaumiza wengine." Huyu ni mtu anayeamini anayo haki kuumiza wengine.

Lakini nilipokea neema kwa sababu nilitenda kwa ujinga katika kutoamini

NI: "Lakini kwa sababu sikuamini katika Yesu, na nilikuwa sijui nilichokuwa nikifanya, nilipokea neema kutoka kwa Yesu"

Nilipokea neema

NI: "Yesu alinionesha neema" au "Yesu kashatoa neema kwangu"

Lakini neema

"Na neema"

ilibubujika kwa imani na upendo

"ilikuwa kwa wingi sana" au "ilikuwa zaidi kuliko ile ya kawaida"

1 Timothy 1:15

Ujumbe huu ni wa kweli

"Kauli hii ni ya kweli"

unaofaa kukubalika

"unaweza kupokelewa bila mashaka yoyote" au "unatakiwa kukubalika kwa ujasiri wote"

kwanza nilikuwa nimepata rehema

"kwanza Mungu alinionesha neema" au "Nilipewa neema kutoka kwa Mungu kwanza"

mfalme mkongwe

"mfalme wa milele" au "mtawala mkuu wa milele"

iwe heshima na utukufu

"aweze kuheshimiwa na kupewa utukufu" au "watu waweze kumweshimu na kukupa utukufu"

1 Timothy 1:18

Nimeweka amri hii mbele yenu

"Amri hii naitoa kwenu" au "Amri hii naiweka kwenu"

mtoto wangu

Hili ni neno la ujumla sana kuliko "mwana" au "binti", lakini bado bado linaonesha uhusiano na baba. Paulo antumia hii kama sitiari kwaajili ya upendo wake kwa Timotheo.

shiriki katika mashindano mazuri

"shiriki katika mashindano ambayo yanafaidisha juhudi" au "jitahidi kuwashinda maadui" Hii ni sitiari ambayo inamaanisha "fanya juhudi kwaajili ya Bwana" (UDB)

amepiga miamba/mawimbi kwa heshima ya imani

Paulo anatumia sitiari nyingine kulinganisha hali ya imani yao na meli ambayo imezama kwenye mwamba. Sitiari hii inamaanisha "kilichotokea kwenye imani zao ambacho ni maafa" (UDB). Utumie hii au sitiari inayofanana kama itaeleweka kwa lugha yako.

wanaweza kufundishwa

"kwamba Mungu anaweza kuwafundisha"

1 Timothy 2

1 Timotheo 02 Maelezo kwa ujumla

Dhana muhimu katika sura hii

Amani

Paulo anawasihi Wakristo kuwaombea kila mtu. Wanastahili kuwaombea viongozi ili Wakristo waishi kwa amani kwa njia ya kimungu na ya kiheshima

Wanawake katika kanisa

Watafsiri wawe makini zaidi ili watafsiri kikamilifi mistari hii.

Maswala mengine ya utata katika tafsiri ya sura hii

"Sala" , "kuombeana" na "shukrani"

Maneno haya yanafanana katika maana yao. Siyo muhimu kuyatazama kama yanayohitilafiana.

<< | >>

1 Timothy 2:1

Kauli unganishi

Paulo anamtia moyo Timotheo kuombwa kwa ajili ya watu wote.

Awali ya yote

"Kitu cha muhimu zaidi" au "Kabla ya kitu chochote"

Nakuomba

"Nakusihi" au "Nakuomba"

Heshima

njia ambayo watu wanaweza kutuheshimu. Iliyoainishwa na "Utauwa", Hii ni njia ambayo watu wengine watamheshimu Mungu na kututii sisi.

1 Timothy 2:5

Mjumbe mmoja kati ya Mungu na mtu

Mjumbe ni mtu anayesaidia kujadili ujumbe wa amani kati ya watu wawili ambao hawaelewani. hapa Yesu anawasaidia wenye dhambikuingia kwenye mahusiano ya Amani na Mungu.

akajitoa mwenyewe

"kufa kwa hiari

Kama fidia

"Kama bei ya uhuru" au "kama malipo ya kupata uhuru"

ushuhuda wa wakati mtimilifu

"Ushuhuda wake ni kwawakati mtimilifu" au "Ushuhuda wa wakati huu"

kwa kusudi hili

"Kwa hii" au "kwa sababu hii" au kwa ushuhuda huu"

nimefanywa kuwa mhubiri

"Nimechaguliwa kuwa mhubiri" au "nimechaguliwa na Kristo kuwa mhubiri"

Natamka ukweli

"Nazungumza ukweli" au "nakuambia ukweli"

Sisemi uongo

"Sidanganyi"

Katika Imani na kweli

"Kuhusu imani na kweli" au "Pamoja na imani na kweli"

1 Timothy 2:8

Kauli unganishi

Paulo anatoa maagizo maalumu kwa wanawake.

wanaume kila mahali

"Wanaume katika kila mahali" au "Wanaume kila sehemu"

Inua juu

"kuongeza"

inueni mikono safi

"Mikono iliyotengwa kwa ajili ya Mungu." hii ni kwa ajili ya mtu anayekwepa dhambi

bila kuwa na hasira wala wasiwasi

"Bila kueleza hasira na mgogoro na wengine" au bila kueleza hasira kuhusu wengine na mashaka juu ya Mungu"

kwa heshima

kwa njia ambayo haitaonyesha kutokuwa na umakini kwao" au "kwa njia ambayo inaonyesha heshima ya wazi kwa watu na kwa Mungu"

si kwa kusuka nywele

"Kufany akazi kwa bidii ili kufanya nywelezionekane kuwasafi". Kusuka nywele ni njia moja ya mwanamke inayompa kutokuwa makini kwenye nywele zake.

wanaokiri uungu kwa kufanya kazi njema

anataka kuonyesha kuwa wao ni mai ya Mungu kwa mambo mazuri wanayoyafanya.

1 Timothy 2:11

katika ukimya

"katika utulivu"

kwakutii

"na wasiulize maswali kuhusu kile wanachokisikia"

simruhusu mwanamke

"simkubalii mwanamke"

1 Timothy 2:13

Adamu aliumbwa kwanza

"Adamu ni mtu wa kwanza ambaye Mungu alimuumba kwanza" au "Adamu aliumbwa kwanza na Mungu"

Baadaye Eva

"Baadaye Eva aliumbwa"

Adamu hakudanganywa

"Na adamu hakuwa wa kwanza kudanganywa na Nyoka"

lakini mwanamke alidanganywa na kukosa kabisa

"Kutotii amri za Mungu kwa sababu alikuwa alikuwa amedanganywa kabisa" lengo kuu katika kifungu hiki ni kuwa alikuwa Eva na siyo Adamu ambaye (Kwanza) hakutii sheria za Mungu.

Ataokolewa kwa kuzaa watoto

"Mungu atamweka salama bila shaka kupitia maisha ya kawaida"

Kama wataendelea

"Kama watabaki" au "Kama wataendelea kuishi"

katika Imani na upendo na utakaso

"Katika kumwamini Yesu na kuwapenda wengine na kuishi maisha matakatifu"

pamoja na uzima na akili njema

"na kuwa na kiasi" au "Na ufahamu wa kujua ni kipi kizuri zaidi"

1 Timothy 3

1 Timotheo 03 Maelezo kwa ujumla

Muundo na Mpangilio

1 Timotheo 3:16 huenda ni wimbo, shairi ama kanuni ya imani kanisa la mwanzo "lililotumia kuorodhesha mafundisho muhimu waumini wote walishiriki.

Dhana muhimu katika sura hii

Waangalizi na Mashemasi

Kanisa lilitumia vyeo tofauti vya viongozi wa kanisa. Vyeo vingine vilijumuisha, mzee, mchungaji na askofu. Neno "Mwaangalizi linaashiria maana ya luga ya awali katika misitari ya 1-2. Paulo anaandika kuhusu "Mashemasi" katika misitari ya 8 na 12 kama aina nyingine ya uongozi wa kanisa.

Maswala mengine ya matata katika tafsiri ya sura hii

Sifa za tabia

Sura hii inaorodhesha sifa chache ambazo lazima mwanaume anayetaka kuwa mwangalizi ama shemasi katika kanisa awe nazo. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-abstractnouns)

<< | >>

1 Timothy 3:1

Kazi njema

Kazi ya kuheshimika

Mume wa mke mmoja

Mwangalizi lazima awe na mke mmoja.Siyo sawa ikiwa hii ninawajumuisha wanaume ambao hapo nyuma walikuwa wajane au wametalikiwa, au hawakuwahi kuoa.

awe na Kiasi

"Asifanye jambo lolote bila kiasi"

Busara

Mtu ambaye anafikiri katika njia ya busara", au"ambaye hutumia sauti ya hukumu"au "busara"mantiki, au "akili"

Mtaratibu

Tabia nzuri

Mkarimu

Mwenye kukaribisha wageni

Asitumie kileo

"Asiwe mlevi" au" asiwe anakunywa sana kileo"

Asiwe mgomvi

"Asiwe mtu ambaye anapenda kupigana na kusemasema"

Asiwe mpenda fedha

Wala mtu ambaye anaiba moja kwa moja au kupitia mitandao siyo mtu ambaye hufanya kazi kwa uwazi kuongeza fedha lakini hajali watu wengine kwa umakini.

1 Timothy 3:4

kwa heshima yote

Maana zinazowezekana ni 1) watoto wa kiongozi waheshimu baba na watu wengine au 2) watoto wa mwangalizi wanapaswa kuwaheshimu watu wote.

Kuongoza nyumba yake

Kuitunza familia yake"au "kulinda watu wanaoishi nyumbani mwake"

Kwa heshima zote

Yote inaweza husika watu wote au katika muda wote au katika shida zozote

Ikiwa mtu hafahamu namna

Kwa sababu ikiwa mtu hafahamu namna ya "au" kwa wakati mtu hawezi "au" lakini kukisia mtu hawezi"

Atawezaje kulitunza kanisa la Mungu

"Hawezi kulitunza kanisa laMungu" au"hatakuwa tayari kuliongoza kanisa la Mungu."

1 Timothy 3:6

Asije akawa mwamini mpya

"Asije akawa mwamini mpya" au " asije akawa mtua mbaye amekuwa mwamini kwa muda mfupi uliopita "au " lazima awe mwamini mchanga"

Asije akaanguka katika hukumu kama mwovu

Kuwa na majivuno kama mwovu anavyofanya na kwa sababu ya kwamba amehukumiwa kama mwovu alivyo.

Lazima pia awe na sifa njema kwa wote wa nje.

"Ni muhimu pia kwa wote ambao hawajamwamini Yesu kufikiri vizuri juu yake"au"Wote wa nje ya kanisa lazima wafikiri vizuri juu yake"

Kuanguka katika aibu

Kuleta aibu juu yake"au"kumpa mtu sababu za kutodhibitishwa kwake"

Kuanguka katika......mtego wa mwovu

Kuruhusu mwovu kumtega." Shetani kutengeneza mtego au kunaswa ni mfano wa shetani kumhadaa kujiingiza katika dhambi bila kujua.

1 Timothy 3:8

Mashemasi vilevile

"Mashemasi, kama kwa waangalizi"

Wawe wakamilifu

Awe anastahili heshima

Asiwe na kauli mbili

Kauli-"siyo kusema kitu kimoja lakini maana ni nyingine"au "siyo kusema kitu kimoja kwa mtu mmoja na kusema vitu vingine tofauti kwa wengine"

Asitumie mvinyo kupita kiasi

"Asitumie mvinyo kupita kiasi"au"asijitoe kutumia mvinyo kupita kiasi"

Wasiwe na tamaa

"Wasiangalie pato lisilo la haki"

Waweze kutunza kweli iliyofunuliwa kwa imani

Lazima waendelee kuamini ujumbe wa kweli uliofunuliwa na Mungu kwetu kwamba tunaamini."Hii inamanisha kwamba kwa kweli iliyoingia kwa muda mrefu lakini Mungu aliionyesha kwao kwa muda huu .

Kwa dhamira njema

"Kwa dhamira njema kujua kwamba hatukufanya chochote kinyume"

Wawe wamedhibitishwa kwanza

Wawe wamedhibitishwa kutadhiminiwa na kuamua ikiwa wanafaa kutumika"au" waweze dhibitisha peke yao kwanza"

Kwa sababu hawana lawama

Ikiwa hakuna mmoja aweza kutafuta chochote kisicho sawa yeye peke yake "au "kwa sababu hawana lawama "au" kwa sababu hawakufanya chochote kisicho sawa"

1 Timothy 3:11

Wanawake vivyo hivyo

Hapa "wanawake"inaweza kutumiwa kama wanawake kwa ujumla, lakini inaonekana inabainisha mashemasi,wake au mashemasi wanawake.Kwenye :"wake vilevile wana mahitaji"au"mashemasi wa kike,pana mahitaji kama mashemasi"

Wawe wakamilifu

"kufanya vizuri"

Wasiwe wasingiziaji

"Ni lazima wasiongee uovu kuhusu watu wengine"

Kiasi

"Wasifanye chochote kwa ziada"

Mume wa mke mmoja

Mtu lazima awe na mke mmoja tu. Siyo sahihi ikiwa hii inajumuisha watu ambao hapo nyuma walikuwa wagane, wamepeana talaka, au hawakuwahi kuoa.

Kutawala vizuri watoto wake na wa nyumbani mwake.

Kutunza na kuongoza vizuri watoto wake na wengine wanaoishi kwenye nyumba yake.

Kwa wote

"Kwa mashemasi wote "au "kwa maaskofu wote. Mashemasi, na mashemasi wa kike"au "kwa viongozi wa makanisa haya"

Wamepata peke yao

"kupokea peke yao "au" kuongezeka peke yao"

1 Timothy 3:14

Kauli Unganishi:

Paulo anamwambia Timotheo sababu iliyomfanya amwndikie barua na kisha anamweleza juu ya uungu wa Kristo.

Na nina tumaini kuja kwako upesi

"ijapokuwa ninatumaini kuja upesi sana"

lakini ikiwa nitachelewa

Lakini ikitokea siwezi kufanya hivyo upesi au "lakini ikiwa kitu chochote kitanizuia kuwa hapo upesi"

katika nyumba ya Mungu

Paulo anaongelea juu ya kikundi cha walioamini kama ni familia moja.

Mungu anayeishi

Msemo huu unamwelezea Mungu kama ndiye atoaye uzima.

Nguzo na mtetezi wa kweli

Paulo anaongea juu ya walioamini na kuibeba kweli kuhusu Kristo kama vile wao ni nguzo na msingi unaoshikilia jengo lote.

1 Timothy 3:16

Katika mwili

Paulo anatumia neno "mwili" hapa kumaanisha Binadamu.

akaonekana na malaika

Hii unaweza pia kusema, "Malaika walimwona"

Alidhibitishwa na Roho

"Roho Mtakatifu alituhakikishia Yesu alikuwa ambaye alisema alikuwa"

alitangazwa kati ya mataifa

"watu wa mataifa mengi waliwaambia wengine kuhusu Yesu"

akaaminiwa kweye ulimwengu

"pande nyingi za ulimwengu zilimwamini Yesu"

1 Timothy 4

1 Timotheo 04 Maelezo kwa jumla

Muundo na mpangilio

1 Timotheo 4:1-3 ni unabii Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#prophet)

Maswala mengine ya utata katika tafsiri ya sura hii

Siku za baadaye

Hii ni njia nyingine ya kuashiria siku za mwisho( Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lastday)

<< | >>

1 Timothy 4:1

Kauli unganishi

Paulo anamwambia Timotheo kile ambacho Roho anasema kitatokea na anamtia moyo kwa kile ambacho anapaswa kufundisha.

nyakati zijazo

Inaweza kumaanisha 1) nyakati za baadaye kuliko nyakati za Paulo, "katika nyakati zinazokuja" au "wakati ujao" au 2) Katika wakati wa Paulo mwenyewe, "katika wakati wa kipindi hiki kabla ya wakati wa mwisho"

kuacha imani

"kuacha kuamini katika Yesu" au "kuondoka katika kile ambacho walikuwa wanakiamini"

kuwa makini kusikiliza

"kutoa kipaumbele" au "kwa sababu wanasikiliza kwa makini" au "wakati wakisikiliza"

roho zidanganyazo na mafundisho ya kipepo

"roho zinazowalaghai watu na mambo ambayo mapepo yanafundisha"

kwa uongo na unafiki

"yanayofundishwa na wanafiki ambao wanawaambia uongo"

dhamiri zao zitakuwa zimechomwa moto

Huu mfano ni wa mabwana ambao walikuwa wakiweka chuma cha moto katika ngozi za watumwa au wanyama kutengeneza kovu ambalo linaonesha umiliki. Yaweza kumaanisha 1) alama ya kuchomwa kama kitu cha kuleta utambulisho, "Wanafanya hivi hata kama wanajiona kwamba ni wanafiki," au 2) dhamiri zao zimetiwa ganzi, "kana kwamba wameweka chuma cha moto katika dhamiri zao kuzifanya kuwa na ganzi"

1 Timothy 4:3

Wata

"Watu hawa wata"

kataza kuoa

"kuwakataza waumini kuoa" au "kuwazuia waumini kuoa"

kataza...kupokea vyakula

"waliwataka watu...wajiepushe na vyakula" au "kuwakataza watu...kula vyakula" au "kutowaruhusu watu...kula aina ya vyakula." "watu" hapa yaweza kumaanisha waamini.

waaminio na waijuao kweli

"waamini waijuao kweli" au "waamini waliojifunza kweli"

hakuna kinachokataliwa kama kitapokelewa kwa shukurani

"hatukitupi kitu chochote ambacho tunamshukuru Mungu kwacho" au "hatukikatai kitu chochote ambacho tunamshukuru Mungu kwacho" au "kila kitu ambacho tunakila kwa shukurani kinakubalika"

kinatakaswa kupitia neno la Mungu na kwa njia ya maombi

tafsiri mbadala: "tumekitenga kwa ajili ya matumizi ya Mungu kwa kulitii neno la Mungu na kumuomba yeye" au "tumekitenga kwa ajili ya matumizi ya Mungu kwa maombi ambayo yanakubaliana na ukweli ambao Mungu ameufunua"

1 Timothy 4:6

kama utayaweka mambo haya mbele ya ndugu

"uweke fikra hizi ndani ya akili za waumini" au "uwasaidie waumini kuyakumbuka maneno haya." "Fikra" au "maneno" yanamaanisha mafundisho.

unaendelea kulishwa

"kufundishwa". Mungu alikuwa akimfanya Timotheo mwenye nguvu na kumfundisha kuyafanya yampendezayo Mungu.

maneno ya imani

"maneno ambayo yanawasababisha au yanayowafanya watu kuamini"

hadithi za kidunia zinazopendwa na wanawake wazee

"hadithi za kidunia na za wanawake wazee." Maneno "zilizopendwa na wanawake wazee" inaweza kuwa mfano kwa maana ya "za kijinga" au "kipuuzi." Paulo hakusudii kuwatukana wanawake katika kuwaongelea kwake :wanawake wazee." Badala yake, yeye na wasikilizaji wake walijua kwamba wanaume wanakufa wakiwa vijana ukulinganisha na wanawake, kwa hiyo kuna wanawake wengi zaidi kuliko wanaume ambao akili zao zimekuwa dhaifu kwa sababu ya umri mkubwa.

jifunze kutenda kwa namna ambayo inampendeza Mungu

"jifunze kuwa wa kiMungu zaidi" au "jifunze kutenda kwa namna ua njia ambayo inampendeza Mungu" au "jitahidi kuwa wa kiMungu zaidi"

mazoezi ya mwili

"mazoezi ya kimwili"

kutakusaidia maisha ya sasa hapa duniani

"ni ya manufaa kwa maisha haya" au "inasaidia kuyafanya maisha haya kuwa bora"

1 Timothy 4:9

wakuaminiwa kabisa

"unastahili imani yako kamilifu" au "unastahili kuamini kwa hali ya juu kabisa"

Ni kwa sababu hii

"Hii ndiyo sababu"

tunafanya kazi kwa bidii na juhudi sana

Maneno "juhudi" na "kufanya kazi kwa bidii" kimsingi yanamaanisha kitu kilekile. Paulo anayatumia yote pamoja kusisitiza ni kwa namna gani wamefanya kazi hiyo kwa bidii.

tumaini letu liko kwa Mungu aishie

"tumeweka tumaini letu kwa Mungu aliyehai"

lakini hasa kwa waaminio

"lakini yeye hasa ni mwokozi kwa wale watu waaminio"

1 Timothy 4:11

Uyaseme na kuyafundisha mambo haya

"Agiza na fundisha mambo haya" au "Agiza na ufundishe mambo haya ambayo nimeyataja hivi punde"

Mtu yeyote asiudharau ujana wako

"mtu asikuchukulie kwamba wewe si wa muhimu kwa sababu u kijana"

endelea kuyasoma

"soma Maandiko" au "endelea kulisoma Neno la Mungu kwa sauti na kwa uwazi mbele za watu"

endelea...kuyahimiza

"wahimize wengine" au "watie moyo wengine kulifanyia kazi Neno la Mungu katika maisha yao"

1 Timothy 4:14

usiache kutumia karama iliyoko ndani yako

Paulo anamzungumzia Timotheo kuwa ni kama chombo ambacho kimebeba karama za Mungu.

usiache

Hii inaweza kutafasiriwa kama, "hakikisha unatumia"

kuwekewa mikono na wazee

Hii ilikuwa ni sherehe ambayo viongozi wa kanisa waliweka mikono juu ya Timotheo na kumuombea kwamba Mungu atamuwezesha kufanya kazi aliyomwamuru au aliyomwagiza kuifanya.

Yafanye mambo hayo yote na uyaishi

"Fanya mambo haya yote na uishi kwa kuyafuata"

ili kukuwa kwako kuwe dhahiri kwa watu wote

"hivyo watu wengine waone ukuwaji wako" au "hivyo watu wengine watauona ubora wa maisha yako kwa kuyafanya hayo"

Dhibiti mwenendo wako

"Enenda kwa uangalifu" au "Dhibiti tabia yako"

Endelea kuyafanya mambo haya

"Endelea kufanya mambo haya"

utajiokoa mwenyewe na watu wanaokusikiliza

"utajiokoa wewe na wale wanaokusikiliza kutoka katika kuamini jumbe za uongo na kufanya matendo mabaya. Watu wanaoamini jumbe za uongo na kufanya matendo mabaya wategemee kutesekea kama matokeo yake. Paulo hataki Timotheo na marafiki zake kuteseka kwa kuamini na kutenda vitu au mambo yasiyo sahihi.

1 Timothy 5

1 Timotheo 05 Maelezo kwa ujumla

Dhana muhimu katika sura hii

Heshima na adabu

Paulo anawahimiza Wakristo wachanga kuwaheshimu na kuwaonyesha adabu Wakristo wazee. Mila huwaheshimu na kuwaonyesha adabu watu wazee kwa njia tofauti.

Wajane

Nyakati za zamani katika Mashariki ya Karibu, ilikuwa ni muhimu kuwasaidia wajane kwa vile hawakuwa na uwezo wa kujipatia chakula.

<< | >>

1 Timothy 5:1

Sentensi unganishi:

Paulo anaendelea kumuasa Timotheo awajali wanaume, wanamke, wajane na wanawake wazee ndani ya kanisa.

Taarifa ya jumla:

Paulo alikua anatoa maagizo haya kwa mtu mmoja, Timotheo.

Usimkemee mwanaume mzee.

"Usiongee kwa ukali kwa mzee wa kiume"

Ila msihi kama baba

"Ila mtie moyo kama uongeavyo na baba yako," kwa adabu.

Msihi kijana wa kiume kama ndugu

"Mtie moyo vijana wa kiume kama ndugu zako" au "wafundishe vijana wakiume kama ambavyo ungefundisha ndugu zako," kwa amani.

Wanawake vijana kama dada

"wasihi wanawake vijana kama ambavyo unge wasihi dada zako" au "wafundishe wanawake vijana kama ambavyo ungewafundisha dada zako,"

Kwa usafi wote

"kwa mawazo safi na matendo" au "katika hali ya utakatifu"

1 Timothy 5:3

Waheshimu wajane

"Waheshimu na kuwahudumia wajane"

wajane kwelikweli

"wajane wasio na mtu wa kuwahudumia"

waache kwanza wajifunze

"awali ya yote wanahitaji kujifunza"

katika nyumba zao wenyewe

kwenye familia zao wenyewe au kwa wale wanaoishi kwenye nyumba zao

waache wawalipe wazazi wao

"Waache wawatendee mema wazazi wao kwa sababu ya mambo mazuri ambayo wazazi wao wamewapa."

1 Timothy 5:5

Lakini mjane halisi ameachwa peke yake

"Lakini yule ambaye ni kweli mjane hana familia"

yeye daima husubiri mbele yake kwa maombi na sala

"husubiri kwa uvumilivu kwa maombi yake na sala"

maombi na sala

maneno haya mawili maana kimsingi yana maana moja. Paulo anayatumia kwa pamoja ili kusisitiza kiasi gani wajane hawa huomba.

usiku na mchana

maneno "usiku" na "siku" hutumiwa pamoja kumaanisha "wakati wote."

Hata hivyo

"Lakini"

wafu

mfano Huu unamaana kwamba yeye hana uwezo wa kumjibibu Mungu. "ni kama mtu aliekufa, hana la kujibu kwa Mungu"

hai

Hii ina maana ya maisha ya kimwili.

yeye daima husubiri kwa maombi na sala

"Anaendelea kufanya maombi na sala"

amekufa

Paulo anaongea kuhusu watu ambao hawamtafuti Mungu na kumpendeza kama walikua wafu. "ni kama mtu aliekufa, hana la kujibu kwa Mungu"

bado yu hai

Hii ina maana ya maisha ya kimwili.

1 Timothy 5:7

Na kuhubiri mambo haya

"Waamuru mambo kama haya vizuri"

ili waweze kuwa na zaidi ya aibu

"hivyo kwamba hakuna mtu anayeweza kupata kosa pamoja nao." Maana ya "wao" ni 1) 'wajane hao na familia zao " au 2)" kanisa. " Ni inaweza kuwa bora kuondoka somo kama "wao."

hatoi kwaajili ya ndugu yake

"haitoi kwa mahitaji ya ndugu zake" au " hatoi msaada kwa mahitaji ya jamaa zake '"

kwa ndugu yake

"kwa ajili ya wanafamilia yake yote" au "kwa wale wanaoishi katika nyumba yake"

kwa wale wa nyumbani kwake

"kwa wanafamilia wanaoishi katika nyumba yake"

ameikana Imani

"yeye ametenda kinyume cha ukweli tunaoukubali"

ni mbaya kuliko mtu asiyeamini

"ni mbaya zaidi kuliko wale ambao hawaamini katika Yesu." Paul anamaanisha mtu huyu ni mbaya kuliko mtu asiyeamini kwa sababu hata wasioamini utunzaji wa ndugu zao. Kwa hivyo, muumini anapaswa atunze ndugu zake.

ili waweze kuwa bila aibu

"hivyo kwamba hakuna mtu anayeweza kupata kosa pamoja nao." Maana ya "wao" ni 1) 'hawa wajane na familia zao "(UDB) au 2)" Waumini. " Ni inaweza kuwa bora kuondoka somo kama "wao."

1 Timothy 5:9

aandikishwe kama mjane

inaonekana kulikuwapo na orodha, iliyoandikwa au la, ya wajane. washiriki wa kanisa waliyatimiza mahitaji hayo ya wanawake ya makazi, mavazi, na chakula; na wanawake hawa walitarajiwa kujitolea maisha yao kwa kuwahudumia jumuiya ya kikristo.

aliye juu ya umri wa miaka sitini

Wajane ambao walikuwa wadogo chini ya miaka sitini wanaweza kuolewa tena, na hivyo Kanisa linapaswa kuwatunza tu wajane ambao walikuwa na umri zaidi ya sitini.

mke wa mume mmoja

Maana inawezekana ni 1) yeye alikuwa daima mwaminifu kwa mumewe au 2) na hajapewa talaka na mume wake na kuolewa na mtu mwingine.

Awe najulikana kwa matendo mema

Hii inaweza andikwa kama "Watu lazima waweze kushuhudia kwa matendo yake mema"

ameniosha miguu

"kufanya kazi kusaidia." Kuosha miguu michafu ya watu ambao wamekuwa wakitembea katika uchafu na matope ni picha ya kukutana na mahitaji ya watu wengine na kufanya maisha yawe yafuraha kwao.

Waaminio

Baadhi ya matoleo hutafsiri "waamini" hapa kama, "Watakatifu" au "watu wa Mungu." Wazo muhimu ni kwa kutaja waumini wa Kikristo.

amefuata kazi zote njema

"ni maalumu kwa ajili ya kufanya matendo mema"

ambaye si mdogo kuliko sitini

Kama Paulo atakapo elezea kwa 5: 11-16, wajane waliokuwa na umri wa miaka midogo kuliko 60 wanaweza kuolewa tena. Kwa sababu hiyo jumuiya ya kikristo walikuwa wakuwatunza wajane ambao walikua na umri zaidi ya miaka sitini.

amekua mkarimu kwa wageni

"amekaribisha wageni katika mji wake"

aliwasaidia watu wenye taabu

Hapa "taabu" linaweza kutumika kama "yeye aliewasaidia wale ambao wanateseka"

amekua akijitoa kwa kila kazi njema

"amejitoa kwa kufanya kila aina ya matendo mema"

1 Timothy 5:11

Lakini kwa habari ya wajane vijana, kataa kuwaandikisha katika orodha

"Lakini msiwaweke wajane vijana kwenye orodha." Orodha ni ya wajane wenye umri wa miaka 60 na zaidi ambao jumuiya ya kikristo ingesaidia.

Kwa kuwa watakaposhindwa na tamaa ya mwili dhidi ya Kristo, watataka kuoa

"ni aliwasihi kutoka kwa Kristo kwa sababu ya tamaa zao za ngono" au "kuwa na tamaa ya mwili inayowafanya watake kutoa dhamira yao ya kiroho"

kutengua ahadi yao ya awali

"wala hawaweki ahadi zao za awali" au "kutokufanya walicho ahidi kukifanya kabla"

dhamira

dhamira ya wajane ilikuwa ni makubaliano yao ya kutumikia jumuiya ya kikristo kwa ajili ya mapumziko ya maisha yao kama jamii angewapa mahitaji yao.

kusengenya

Hawa ni watu ambao hujadili juu ya maisha binafsi ya watu wengine.

mambo wasio paswa kusema

"mambo ambayo si sahihi hata kutaja"

kuwa wamezoea kuwa wavivu

"kuingia katika tabia ya kutokufanya kitu

1 Timothy 5:14

kusimamia nyumba

"kumhudumia kila mtu katika nyumba yake"

wameshamgeukia Shetani

Paulo anazungumzia wanaoishi katika uaminifu kwa Kristo kana kwamba ni njia ya kufuatwa. Hii ina maana mwanamke aliacha kumtii Yesu na kuanza kumtii Shetani. "kuacha njia ya Kristo na kumfuata Shetani" au "aliamua kumtii Shetani badala ya Kristo"

mwanamke yeyote aaminie

"mwanamke yeyote Mkristo" au "mwanamke yeyote ambaye anaamini katika Kristo"

anao wajane

"anao wajane katika jamaa yake"

wajane kweli

"wale wanawake ambao hawana mtu wa kutoa kwa ajili yao"

adui

Inawezekana Maana ni 1) hii inamaanisha Shetani au 2) hii inamaanisha wasio amini.

ili kanisa lisilemewe

Paulo anazungumzia jamii kuwa inasaidia zaidi watu kuliko uwezo wao kama walikuwa wamebeba uzito juu ya migongo yao. Hii inaweza kusemwa "ili kwamba jumuiya ya kikristo haitawasaidia wajane ambao familia inaweza kutoa kwa ajili yao"

1 Timothy 5:17

Sentensi uanganishi:

Paulo tena anazungumzia jinsi wazee (maaskofu) wanapaswa kutunzwa na kisha kumpa Timotheo maelezo binafsi.

watambue wazee wanaoongoza vyema

"Ninyi waumini wote mnapaswa kufikiri kama mnastahili"

Heshima mara mbili

Maana inawezekana ni 1) "ya heshima na malipo" au 2) "heshima zaidi kuliko wengine wapokeavyo"

wale wanaofanya kazi na neno na katika kufundisha

"wale wanaohubiri na kufundisha neno la Mungu"

kufunga

kifaa kianachowekwa kwenye pua na mdomo wa mnyama ili kumzuia kula wakati anafanya kazi.

kupura nafaka

Hii ni njia ya kutenganisha nafaka na makapi kwa kutumia mkokoteni unaovutwa na ng'ombe

anastahili

"inastahili"

1 Timothy 5:19

usipokee mashitaka

Paulo anaongea juu ya mashitaka kama vitu ambavyo vinaweza kushikika au kupokelewa na watu

mbili au tatu

"angalau mbili" au "mbili au zaidi"

wenye dhambi

hii inahusu mtu yeyote kufanya jambo lolote ambalo halimtii au yasiyompendeza Mungu, hata mambo ambayo watu wengine hawayajui.

mbele ya watu wote

"ambapo kila mtu anaweza kuona"

ili wengine wawe na hofu

"ili wengine waweze kuogopa kufanya dhambi"

1 Timothy 5:21

malaika wao wateule

Hii inamaanisha malaika ambao Mungu na Yesu wamewachagua kuwatumikia wao kwa njia maalumu.

weka mikono

Hii ilikuwa sherehe ambapo viongozi wa kanisa moja au zaidi wangeweka mikono juu ya watu na kuomba kwamba Mungu aweze kuwawezesha watu hao kutumikia kanisa kwa njia ambayo Mungu angekuwa radhi. Timotheo alikuwa anasubiri hadi mtu aoneshe tabia nzuri kwa muda mrefu kabla ya kumweka rasmi mtu huyo kuitumikia jamii ya Kikristo.

usishiriki katika dhambi ya mtu mwingine

"kujiunga katika dhambi ya mtu mwingine." Maana inawezekana ni 1) kama Timotheo akichagua mtu ambaye ana dhambi na kuwa mfanyakazi wa kanisa, Mungu angemshikilia Timotheo kuwajibika kwa dhambi ya mtu huyo, au 2) Timotheo hapaswi kutenda dhambi akiona wengine wakitenda.

tunza amri hizi bila ya kuathiri na kwamba wewe usifanye kitu nje ya upendeleo

kwa maneno "upendeleo," Paulo anasisitiza kwamba Timotheo lazima ahukumu kwa uaminifu na kuwa wa haki kwa kila mtu. "kwamba ushike sheria hizi bila ya kuwa sehemu au kuonesha upendeleo kwa mtu yeyote"

tunza amri hizi

Maana inawezekana ni 1) hii inamaanisha sheria ambazo Paulo amemwambia Timotheo au 2) hii inamaanisha sheria ambazo Paulo anataka kumwambia Timotheo.

1 Timothy 5:23

Usinywe maji tena

Au "Unapaswa kuacha kuwa mnywaji wa maji," anaekunywa maji tu. Paulo hakatazi maji. Anapendekeza ya kwamba Timotheo atumie mvinyo kama dawa. Maji ya eneo lile husababisha madhara mara kwa mara.

Na huwatangulia hukumuni

"dhambi zao hutangulia mbele ya watu hao hukumuni."

lakini baadhi ya dhambi hufuata baadaye

"Lakini baadhi ya dhambi hufuata watu hao baadaye." Maana inawezekana ni 1) Timotheo hatajua kuhusu baadhi ya dhambi mpaka baadaye, au 2) Kanisa hawataweza kujua kuhusu baadhi ya dhambi mpaka baadaye, au 3) Mungu hata hukumu baadhi ya dhambi mpaka hukumu ya mwisho.

nzuri

Hapa "nzuri" ina maana wao wanaolingawa na tabia ya Mungu, makusudi yake, na mapenzi.

hata wengine hawawezi kujificha

"matendo mema mengine yatajulikana katika siku zijazo"

dhambi za baadhi ya watu zinajulikana wazi

Hii inaweza semwa kama "Dhambi za watu wengine ni dhahiri sana"

baadhi ya matendo mema yanajulikana wazi

"baadhi ya matendo mema ni dhahiri"

1 Timothy 6

1 Timotheo 06 maelezo kwa jumla

Dhana muhimu katika sura hii

tumwa

Paulo hasemi katika sura hii iwapo utumwa ni mzuri ama ni mbaya. Paulo anaandika kuhusu kuwaheshimu na kuwatumikia kikamilifu mabwana zao. Paulo anawafunza waumini wote kuwa na uungu na kutosheka katika kila jambo.

__<< | __

1 Timothy 6:1

Sentensi unganishi

Paulo anatoa maagizo maalumu juu ya watumwa na bwana zao kisha maelekezo ya namna ya kuishi maisha ya kimungu.

wale wote walio chini ya nira kawa watumwa

Paulo anaongea juu ya watu wanaofanya kazi kama watumwa kwamba ni kama ng'ombe wanaobeba nira

wale wote

kwa kauli hii Paulo anamaanisha walioamini

jina la Mungu

hii inamaanisha asili ya Mungu, au tabia yake

1 Timothy 6:3

afundishaye kwa upotovu

anayefundisha mapokeo tofauti

liongozalo kwenye utaua

inayowasaidia watu kufanya yaliyo ya Mungu

akili zilizoharibika

akili zilizojaa uovu

wanaiacha kweli

kuacha maana yake ni kuacha kufanya kitu

1 Timothy 6:6

utaua na kuridhika ni faida kubwa

ni faida kubwa kwa mtu kufanya mapenzi ya Mungu na kuridhika na alicho nacho

ni faida kubwa

inatupatia faida kubwa au inatufanyia mambo mengi mazuri.

1 Timothy 6:9

kuwa na mali huanguka katika majaribu, katika mtego

Paulo anaongea juu ya wale ambao vishawishi vya pesa vinawafanya waangukie katika shimo ambalo mwindaji amelitumia kama mtego

Huanguka katika upumbavu mwingi na tamaa mbaya

huu ni mwendelezo wa fumbo la mtego. Hii inamaanisha kuwa tamaa zao za kijinga na mbaya zitawashinda.

watu ambao hutamani hiyo

wanaotamani fedha

1 Timothy 6:11

Bali wewe

Hapa "wewe" ipo katika umoja na inamaanisha Timotheo

mtu wa Mungu

mtumishi wa Mungu

huru mabali na hivi vitu

Paulo anaongea juu ya majaribu na dhambi kama vitu ambavyo mtu angeweza kuvikimbia

ulitoa ushuhuda

ulishuhudia

mbele ya mashahidi wengi

Paulo anaelezea wazo la eneo fulani ili kuonesha watu ambao Timotheo aliongea nao.

1 Timothy 6:13

Sentensi unganishi:

Paulo anaongea juu ya ujio wa Kristo, anatoa maelekezo stahiki kwa matajiri, na mwisho anamaliza na ujumbe muhimu kwa Timotheo.

Nakupa amri hii

Hivi ndivyo ninavyokuamuru

mbele ya Mungu

katika uwepo wa Mungu. Inaonekana ni kama Paulo anamwomba Mungu kuwa shahidi wake

mbele ya Kristo

katika uwepo wa Kristo. Inaonekama ni kama Paulo anamwomba Yesu kuwa shahidi wake

pasipo mashaka

Maana tarajiwa 1) Yesu hataona kosa kwa Timotheo au 2) watu wengine hawataona kosa kwa Timotheo

ujio wa Bwana wetu Yesu Kristo

mpaka Bwana wetu Yesu Kristo atakapokuja tena

1 Timothy 6:15

Mungu atadhihirisha ujio wake

Hii inaweza kumaanisha kuwa Mungu atamdhihirisha Yesu

kwa wakati sahihi

kwa wakati unaofaa/muafaka

mbarikiwa

Anayestahili sifa. Hii inamaanisha Mungu Baba

Peke yake anaishi milele

Yeye pekee ana nguvu ya kuishi milele

akaaye katika mwanga usiokaribiwa

anakaa katika mwaka unaong'aa sana ambao hakuna awezaye kuukaribia

1 Timothy 6:17

waambie matajiri

Hapa "matajiri" kisifa. Inaweza kutafasiriwa kama, waambie wote walio matajiri.

katika utajiri, ambao siyo wa uhakika

katika vitu vingi wanavyovitumaini ambavyo wanaweza kuvipoteza

utajiri wote wa kweli

vitu vyote ambavyo vitatufanya kuwa na furaha ya kweli. Kama vile, upendo, furaha, na amani

watajirike katika kazi njema

Paulo anaongea juu ya baraka za rohoni kama vile ni utajiri wa duniani.

1 Timothy 6:20

linda kile ulichopewa

kwa uaminifu hubiri ujumbe wa kweli ambao Yesu amekupa

epuka majadiliano ya kipumbavu

usitilie maanani majadiliano yasiyofaa

ambayo kwa uongo huitwa maarifa

ambayo kwa ujinga watu wengine huyaita maarifa

wameikosa imani

Paulo anazungumzia imani katika Kristo kama vile shabaha yetu

Neema na iwe pamoja nawe

Mungu awape neema ninyi nyote. Neno "ninyi" limetumiwa katika wingi na linarejelea jamii yote ya Wakristo.

Utangulizi wa 2 Timotheo

Sehemu ya 1 Utangulizi wa jumla

Muhtasari wa Kitabu cha 2 Timotheo

  1. Paulo anamsalimia Timotheo na kumshauri kuvumilia mateso anapomtumkia Mungu (1:1-2:13).
  2. Paulo anampa Timotheo maelekezo ya kibinafsi (2:14-26)
  3. Paulo anamuonya Timotheo kuhusu matukio yajayo na anamshauri jinsi ya kutekeleza kazi yake kwa Mungu (3:1-4:8)
  4. Paulo anatoa matamshi ya kibinafsi

Nani aliandika kitabu cha 2 Timotheo?

Paulo aliandika kitabu cha 2 Timotheo akiwa gerezani Roma. Hapo awali alijulikana kama Saulo. Alitokea mji wa Tarso. Kabla ya kuwa Mkristo alikuwa Mfarisayo na alikuwa akiwatesa sana Wakristo. Baada ya kuwa Mkristo, alisafiri mara nyingi katika himaya nzima ya Warumi akiwahubiria watu kumhusu Yesu.

Hii ni barua ya pili ya Paulo kwa Timotheo. Timotheo alikuwa mwanafunzi wake na rafiki wake wa karibu. Paulo aliandika barua hii akiwa gerezani Roma.Paulo alikuwa karibu kufa.

Kitabu cha 2 Timotheo kinahusu nini?

Paulo alikuwa amemwacha Timotheo katika mji wa Efeso ili awasaidie waumini huko. Paulo aliandika barua hii kushauri Timotheo kuhusu maswala kadhaa. Maswala aliyozungumzia katika barua hii yalikuwa: onyo kuhusu walimu wa uwongo na kuvumilia katika nyakati za matatizo. Barua hii inaonyesha jinsi Paulo alikuwa anamuandaa Timotheo kuwa kiongozi wa makanisa.

Kichwa cha kitabu hiki kitafsiriwe namna gani?

Watafsiri wanaweza amua kukiita kitabu hiki kutumia jina la asili "2Timotheo" ama wanaweza tumia kichwa cha kueleweka zaidi kama "Barua ya Pili ya Paulo kwa Timotheo", ama "Barua ya Pili Kwa Timotheo."(Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-names)

Sehemu ya 2 Dhana muhimu za kidini na kitamaduni

Ni taswira gani ya mwanajeshi katika 2 Timotheo?

Paulo aliposubiri gerezani akiwa anafahamu kuwa angekufa muda si mrefu, alizungumzia mara nyingi kumhusu mwenyewe kama mwanajeshi wa Kristo. Wanajeshi huwajibika kwa amiri yao jinsi Wakristo wajibikao kwa Kristo. Kama "wanajeshi" wa Kristo, waumini wanapaswa kuheshimu amiri zake hata kama kufanya hivyo kutapelekea hao kufa.

Nini maana ya maandiko kuwa pumzi ya Mungu?

Mungu ndiye mwandishi halisi wa maandiko. Aliwaongoza waandishi binadamu. Hii ina maana kwamba kwa namna moja Mungu alisababisha uandishi wa maandiko na watu. Hii ndiyo maana maandiko yanajulikana pia kama neno la Mungu.Hii inamaanisha vitu vingi kuhusu Bibilia. Kwanza ni kwamba Bibilia haina kasoro na inaweza kuaminiwa. Pili, tunaweza kumtegemea Mungu kulinda maandiko kutokana na wale wanaotaka kuyaharibu. Tatu, neno la Mungu linafaa litafsiriwe katika lugha zote za dunia.

Sehemu ya 3: Maswala muhimu ya tafsiri

Umoja na wingi wa "wewe/nyinyi"

Neno "mimi" katika kitabu hiki linaashiria Paulo. "Wewe" inamaanisha Timotheo. Tofauti ya haya ni 4:22 (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-exclusive and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-you)

Paulo alimaanisha nini na maelezo "ndani ya Kristo" na "ndani ya Bwana" na kadhalika?

Paulo alitaka kuelezea wazo la kuwa na ushirika wa karibu sana kati ya muumini na Kristo. Tafadhali tazama utangulizi wa kitabu cha Warumi kwa maelezo zaidi kuhusu kauli hii.

Ni maswala gani kuu ya kimaandishi katika kitabu cha 2 Timotheo?

Katika aya zifuatazo,matoleo ya kisasa yanatofautiana na matoleo ya kale. Toleo la ULB lina masomo ya kisasa na imeweka masomo ya zamani kwenye tiniwayo(maelezo ya chini). Iwapo tafsiri ya Bibilia inapatikana eneo kwa ujumla, watafsiri wanashauriwa kuzingatia matumizi ya masomo yaliyoko katika matoleo hayo. Kama sivyo, watafsiri wanashauriwa kutumia masomo ya kisasa.

(See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/jit.html#translate-textvariants)

2 Timothy 1

2 Timotheo 01 Maelezo kwa jumla

Dhana muhimu katika sura hii

Watoto wa kiroho

Paulo alimfundisha Timotheo kuwa Mkristo na kiongozi wa kanisa. Kuna uwezekano kwamba Paulo pia alimuongoza kumwamini Kristo. Kwa maana hiyo Paulo anamwita Timotheo (Mwanangu mpendwa" (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#disciple and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#spirit))

Maswala mengine ya utata katika kutafsiri sura hii

Mateso makali

Paulo alikuwa gerezani wakati akiandika barua hii. Paulo anamhimiza Timotheo kuwa tayari kuteseka kwa sababu ya injili. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

| >>

2 Timothy 1:1

Paulo

"Toka kwa Paulo" au "Mimi, Paulo, naandika barua hii"

Kwa mapenzi ya Mungu

"kwa sababu ya mapenzi ya Mungu" au "kwa sababu Mungu anataka." Pauli alikuwa mtume kwa sababu Mungu alitakaPaulo awe mtume sio kwa sababu wanadamu walimchagua.

Sawasawa na

Inaweza kuwa na maana 1)"kuweka pamoja na," ikimaanisha kama Mungu alivyoahidi kuwa Yesu uhai, alimfanya Paulo kuwa mtume au 2) "kwa kusudi la,"ikimaanisha kuwaMungu alimteua Paulo kuwaambia wengine kuhusu ahadi ya Mungu ya uhai katika Yesu.

Ahadi ya uhai iliyo ndani ya Yesu Kristo

"Mungu aliahidi kuwafanya wale waliondani ya Kristo Yesu kuwa hai"

Mwana mpendwa

"mwana mpenzi" au "mwana apendwaye" au "mwana ninayempenda." Timotheo aliokolewa na Kristo kwa kupitia Paulo, na hivyo Paulo anamchukulia kama mtoto wake.

Neema, rehema, na amani toka

"Na neema, rehema na amani iwe kwako toka" au " Na upate neema, rehema, na amani toka"

Mungu Baba

"Mungu ambaye ni Baba yetu"

Na Kristo Yesu Bwana wetu

"na Kristo Yesu ambaye ni Bwana wetu"

Maelezo ya jumla.

Kwenye kitabu hiki neno "sisi" inawazungumzia Paulo na Timotheo pamoja na waamini wote.

2 Timothy 1:3

Ninayemtumikia, kama mababa zangu walivyofanya

Paulo alimwabudu Mungu yuleyule ambaye mababu zake walimwabudu. "...ambaye ninafanya majukumu yangu kama Mkristo kama mababu zangu waliokuja kabla yangu walivyofanya"

Kwa nia njema

"kwa nia safi." Hasumbuliwi na fikra za matendo maovu kwa sababu kila mara alijaribu kufanya yaliyo mema.

Ninapowakumbuka ninyi

"Ninapowakumbuka ninyi kila mara" au "ninapowakumbuka kila wakati"

Usiku na

inaweza kuwa na maana 1) "maombi yangu usiku na mchana" au 2) "Ninawakumbuka kila mara usiku na mchana" au 3) "natamani kuwaona usiku na mchana."

Natamani kukuona

"nasubiri sana kukuona"

Nakumbuka machozi yako

"naweka mambo yote yanayokutesa kwenye akili yangu"

Nijawe na furaha

"niwe na furaha sana" au "nifurahie"

Naikumbuka

"kwa sababu nimekuwa nikiikumbuka" au "nilipokuwa nikiikumbuka" au "kwa kuwa naikumbuka"

Imani yako iliyo thabiti

"imani yako ya kweli" au "imani isiyo ya unafiki." inamaanisha kutokuficha kitu au kuwa mkweli.

imani... iliyokuwa kwanza kwa bibi yako... ipo kwako pia

Bibi yake na Timotheo alikuwa mwanamke mcha Mungu, na Paulo anaifananisha imabi ya Timotheo na ya bibi yake.

Loisi ... Yunisi

Haya ni majina ya wanawake.

2 Timothy 1:6

Maelezo yanayounganisha:

Paulo anamtia moyo Timotheo kuishi kwa nguvu, upendo, nidhamu na kutokuona aibu kwa sababu ya mateso ya Paulo gerezani kwa sababu ya imani ya Paulo kwa Kristo.

Hii ndiyo sababu

"Kwa sababu hii" au "Kwa sababu ya imani yako ya kweli kwa Yesu" au "Kea sababu una imani ya kweli kwa Yesu"

Nakukumbusha

"Nakukumbusha wewe" au "Nakwambia tena wewe"

fufua karama ya Mungu iliyo ndani yako kwa kuwekewa mikono yangu

Paulo alimuwekea Timotheo mikono, kumkabidhi roho mtakatifu na uwezo wa kiroho au zawadi juu yake. Paulo anamwambia "afufue" ule uwezo wa kiroho kwenye kazi zake kwa ajili ya Kristo.

Kwa kuwa Mungu

"Sababu Mungu"

Mungu hakutupa roho ya woga lakini ya nguvu na upendo na nidhamu.

Paulo alipokea roho toka kwa Mungu. Alipoweka mikono yake juu ya Timotheo, roho yule yule alikuja juu ya Timotheo. Roho huyu hakusababisha wamuogope Mungu au watu wengine.

Roho wa ... nidhamu

Inaweza kumaanisha "Roho wa mungu anaweza kuwasaidia kujizuia wenyewe" au 2) "Roho wa Mungu anatusaidia sisi kuwarekebisha wengine wanaofanya makosa."

2 Timothy 1:8

Ushuhuda

"kushuhudia" au "kuwaambia wengine"

Ushiriki mateso kwa ajili ya injili

Paulo aliteseka kimakosa kwa ajili ya injili. Anamwambia Timotheo asiogope kuteseka kwa ajili ya ijnili.

Sawasawa na nguvu za Mungu

"Kumruhusu Mungu kukupa nguvu"

Sio kwa ajili ya kazi zetu

"Sio kwa sababu ya mambo mengi mazuri tuliyoyafanya tummeokolewa" au " Mungu hakutuokoa kwa sababu ya mambo mazuri tuliyoyafanya" au "Mungu alituokoa japokuwa tulifanya mambo mabaya"

Aliyetuokoa kwa mipango yake mwenyewe

"Mungu alipanga kutuokoa na sasa ametuokoa" au "Mungu aliamua kutuokoa ni vipi atatuokoa na sasa ametuokoa" au "aliyetuokoa... kama alivyopanga"

Tangu mwanzo

"Kabla ulimwengu haujaanza" au "kabla ya mwanzo"

wokovu wa Mungu umefunuliwa kwa kuja kwa mwokozi wetu Yesu Kristo

"Mungu ameonyesha namna ambavyo anaweza kutuokoa kwa kutupa mkombozi wetu Masihi Yesu kufunuliwa"

Aliyeondoa mauti

"Aliyeondoa nguvu ya kifo juu yetu"

kuleta uzima usiokwisha kwenye mwanga katika injili

"Kufundisha ni maisha gani yasiyokuwa na mwisho kwa kuhubiri injili"

Niliteuliwa kuwa muhubiri

"Mungu alinichagua kuhubiri ujumbe"

Mtumwa wake

"mtumwa kwa ajili yake" au "mtumwa kwa sababu nashuhudia habari za Bwana"

kwa Kristo Yesu

"kupitia mahusiano Yetu na Kristo Yesu"

kwa wito mtakatifu

"Tumetengwa kuwa watu wake kwa wito mtakatifu" au "kuwa watu wake watakatifu"

Alifanya haya

"alituokoa na kutuita sisi"

Kwa kuja mkombozi wety Kristo Yesu

"kwa kumtuma mkombozi wetu Yesu Kristo."

2 Timothy 1:12

Kwa sababu hii

"Kwa sababu mimi ni nabii"

Nateseka pia

Paulo anaelezea namna alivyo mfungwa.

Nina hakika

"Nina shawishika"

Siku ile

Inaweza kuwa na maana ya 1) Siku ambayo Bwana atakuja tena au 2) siku ambayo Mungu atawahukumu watu.

Utunze mfano wa ujumbe wa uaminifu uliousikia toka kwangu

"Endelea kufundisha mawazo ya kweli niliyokufundisha" au "tumia maneno yangu ma mafundisho yangu kama mfano kwa utakachofundisha"

Hilo jambo zuri

Hii inaelezea kazi ya kutangaza injili kwa usahihi.

Yatunze

Timotheo anatakiwa kuwa makini na watu wanaopinga kazi yake, wanajaribu kumkataza na kupinga nachokisema.

Kupitia roho mtakatifu

"Fanya yote na yale ambayo roho mtakatifu amekwambia uyafanye"

2 Timothy 1:15

Wameniacha

Walimuacha kwa kuwa alikuwa amekamatwa na kutupwa gerezani.

Hawakuionea aibu minyororo yangu

Onesiphorus hakumuonea aibu Paulo kwa sababu alikuwa gerezani ila alienda kumtembela mara kwa mara. "minyororo" inaelezea mtu aliyeko gerezani.

Mungu amjalie kupata neema... siku ile

Paulo anatamani Onesiphorus apokee neema na sio adhabu au 1)Siku Bwana akija tena au 2) Siku ambayo Mungu atawahukumu watu.

Figelo na Hemogene... Onesiforo

Haya ni majina ya watu.

kwenye nyumba

"kwa familia"

kupata rehema kutoka kwake

Paulo anazungumza kuhusu rehema kuwa ni jambo la muhimu la kutafta.

Siku ile

Hii inaelezea siku ambayo Mungu atawahukumu watu.

2 Timothy 2

2 Timotheo 02 Maelezo kwa Ujumla

Muundo na mpangilio

Matoleo mengine yanaweka maneno kulia kwa ukurasa kuliko maandishi mengine. ULB hufanya hivi na aya za 11-13 kuliko aya zingine. Huenda Paulo ananukuu shairi ama wimbo katika mistari hii.

Dhana muhimu katika sura hii

"Tutatawala naye

Wakristo waaminifu watatawala pamoja na Kristo siku zijazo. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faithful)

Mifano muhimu ya usemi katika sura hii

Mifano

Katika sura hii, Paulo anatumia mifano nyingi kufundisha maisha ya kikristo. Anatumia mifano ya mwanajeshi, mwanariadha na mkulima. Baadaye anatumia mifano ya aina nyingi ya vyombo vya nyumbani.

<< | >>

2 Timothy 2:1

Kuunganisha Maelezo

Paulo alipigapicha maisha ya Kikristo ya Timotheo kama maisha ya askari, kama maisha ya wakulima, kama maisha ya mwanamichezo

kuimarishwa katika neema iliyo katika Kristo Yesu

Maana inawezekana ni 1) 'basi Mungu kutumia neema akawapa kwenu katika Kristo Yesu kuwafanya kuwa imara (UDB) au 2) 'kuhamasisha mwenyewe, wakijua kwamba Mungu amewapa ninyi neema ambayo huja tu kwa njia ya Kristo Yesu

kati ya mashahidi wengi

"na mashahidi wengi kuna kukubaliana kwamba maneno yangu ni kweli"

mwaminifu

"kuaminika"

mwanangu

Paulo anamuona Timotheo kama mtoto wake kwa kuwa alimfundisha Timotheo kumwamini Kristo. "aliye kama mtoto wangu"

uyakabidhi kwa watu waaminifu

Paulo anatoa maelekezo kwa Timotheo kuwa ayakabidhi kwa watu waaminifu ili wayatumie kwa usahihi. "wafundishe"

2 Timothy 2:3

Shiriki mateso nami

Maana inawezekana ni 1) 'kuvumilia mateso kama mimi' (UDB) au 2) 'kushiriki katika mateso yangu'

Hakuna askari atumikae wakati akijihusisha na shughuli za maisha haya

"Hakuna askari atumikae wakati yeye hushiriki katika shuughuli ya kila siku ya maisha haya" au 'Wakati askari wanatumikia, hawana kupata mambo ya kawaida ambayo watu kufanya" watumishi wa Kristo lazima wasiruhusu maisha ya kila siku kuwaweka kutoka kufanya kazi kwa Kristo

Kama askari mzuri wa Kristo Yesu

Paulo anayafananisha mateso kwa ajili ya Kristo Yesu na mateso anayoyavumilia askari mzuri"

Afisa mkuu

"mmoja wapo aliyempendekeza yeye kama askari

mwanamichezo.... si taji isipokuwa awe ameshindana kwa sheria

watumishi wa Kristo inahitajika kufanya kile ambacho Kristo anasema kifanyike.

yeye sio taji isipokuwa awe ameshindana kwa sheria

"Wao watamvika taji yeye kama mshindi pekee ikiwa ameshindana kwa sheria

yeye hatapewa taji

"yeye hakusinda tuzo"

Kushinda kwa sheria

"Inashindana kwa mujibu wa sheria" au "madhubuti kumt'ii sheria"

wakati huo huo akijihusisha

Paulo anazungumzia uharibifu huu kama vile mtego unaowatega watu wakiwa wanatembea.

2 Timothy 2:6

Mkulima mwenye bidii apokee ujira wa mazao yake kwanza

Huu ni mfano wa tatu kwamba Paulo anampa Timotheo, msomaji anapaswa kuelewa kuwa watumishi wa Kristo wanahitaji kufanya kazi kwa bidii.

Fikiria juu ya ninachosema

Paulo alimpa Timotheo neno la picha, lakini hakuweza kabisa kuelezea maana zake, Yeye anatarajia Timotheo kufikiri nini alikuwa akisema kuhusu watumishi wa Kristo.

kwa maana Bwana

kwa sababu Bwana

Kwa kila kitu

"kuhusu vitu vyote"

2 Timothy 2:8

Kuunganisha maelezo

Paulo anatoa maelekezo Timothy juu ya jinsi ya kuishi kwa ajili ya Kristo, jinsi ya kuteseka kwa ajili ya Kristo, na jinsi ya kuwafundisha wengine kuishi kwa ajili ya Kristo.

kulingana na ujumbe wangu wa injili

kama ujumbe wangu wa injili usemavyo

ambavyo mimi nateseka

"kwa ambavyo mimi nateseka

hata kufungwa minyororo

"Kufungwa" inamaanisha kuwa gerezani.

Neno la Mungu haliwezi kulifungwi minyororo

"si vikwazo" au "si kufungwa" "ana uhuru kamili"

kwa wale ambao wamechaguliwa

"kwa watua ambao Mungu amewachagua"

wapate wokovu

"watapokea wokovu"

Utukufu wa milele

"Wanamtukuza Mungu milele" au "akizungumzia watu kwa Mungu milele"

Toka kwa uzao wa Daudi

"uzao" linamaanisha kizazi. "Ambao ni kizazi cha Daudi"

ambaye alifufuliwa kutoka kwa wafu

"Ambaye Mungu alimfufua"

2 Timothy 2:11

Msemo huu

"maneno haya"

Kufa

Hapa hii ina maana mtu kufa kwa nafsi yake. Kwa maneno mengine, kukataa kutoka katika tamaa yake mwenyewe.

tusipokuwa waaminifu

"hatakama tunamkosea Mungu" au "hatakama hatuwezi kufanya nini tunaamini Mungu anataka tufanye"

Yeye hawezi kujikana mwenyewe

"Yeye lazima daima hutenda kulingana na tabia yake" au "hawezi kutenda katika njia ambazo ni kinyume cha tabia yake halisi"

Ikiwa tumekufa pamoja naye ... hawezi kujikana mwenyewe

Hii ni kama wimbo au shairi ambalo Paulo ananukuu. Kama kwenye lugha yako kuna namna ya kuielezea kama shairi unaweza kutumia hapa. Kama hamna unaweza kutafsiri kama sentensi na sio shairi.

2 Timothy 2:14

maelezo ya jumla

Neno "ninyi" linaweza kuwa na maana ya 1) "Waalimu" (UDB) au 2) "watu wa Kanisa"

mbele za Mungu

'Katika uwepo wa Mungu' au 'wakijua kwamba Mungu hukuangalia wewe na hao'

si kwa ugomvi kuhusu maneno

"Si kujadiliana juu ya nini maana ya maneno" au "si kusema maneno ambayo kusababisha mapigano" au "si kusema maneno yenye maana ya kuumiza wengine"

haufai kitu

"hakuna yoyote mzuri" au "asiye na maana"

yanaangamiza

picha ni ya uharibifu wa jengo hilo. Wale ambao husikia ugomvi kuacha kuheshimu ujumbe wa Kikristo

kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu

"kujionyesha kwa Mungu kama mtu umeonyesha kuwa unastahili"

kama mfanyakazi

"Kama mfanyakazi" au "kama mfanyakazi"

utunzaji kwa usahihi

usahihi kuelezea

2 Timothy 2:16

Neno lao kuenea kama donda ndugu

"Nini wanasema yataendelea kusambaa kama ugonjwa wa kuambukiza" Kama vile donda ndugu kuenea katika mwili wa mtu na kuuteketeza, nini watu hao walikuwa wakisema ingeweza kuenea kutoka mtu hadi mtu na kudhuru imani ya wale ambao walisikia maneno hayo, "neno lao kuenea haraka na kusababisha uharibifu kama donda ndugu" au "Watu haraka kusikia wanayoyasema na kuwa wanaathirika nayo

Donda ndugu

wafu, huozo mwili. njia pekee ya kuweka donda ndugu kueneza na kumuua mtu mgonjwa ni kwa kukatwa eneo lililoathirika.

ufufuo ulishafanyika

Mungu tayari amewafufa waumini waliokufa kwenye uzima wa milele '

kubadirisha imani ya watu wengine

Kufanya baadhi ya waumini kuwa na shaka' au "kushawishi baadhi ya waumini kwa kuacha kuamini"

ambayo huongoza kwa zaidi na zaidi ya uasi

"inayoweza kusababisha watu wakawa kinyume na Mungu"

Himenayo na Fileto

Haya ni majina ya wanaume.

walioukosa ukweli

Paulo anazungumzia ukweli kama lengo kuu. Paulo anamaanisha watu hawa hawajaelewa ukweli na wanafundisha uongo.

2 Timothy 2:19

Msingi wa Mungu

Maana inawezekana ni 1) "Kanisa la Mungu limejenga tangu mwanzo" au 2) "ukweli juu ya Mungu" (UDB) au 3) "uaminifu wa Mungu."

anaetaja jina la Bwana

ambaye anasema yeye ni muumini katika Kristo

Aachane na uovu

Maana inawezekana ni 1)"kuacha kuwa mbaya" au 2) "kuacha kufanya mambo yasiyofaa.'"

Vyombo

Hii ni neno la ujumla kwa bakuli, sahani, sufuria, ambayo watu kuweka chakula au kinywaji humo. Kama lugha yako haina neno la ujumla, kutumia neno kwa 'bakuli' au 'sufuria.' Ni mfano kwa ajili ya watu

Heshima.... kutokuheshimu

Maana inawezekana ni 1) 'hafla maalum ... kawaida mara' (UDB) au 2) 'aina ya shughuli watu wema kufanya hadharani ... aina ya shughuli watu wema kufanya binafsi.'

ajitakase mwenyewe kutoka matumizi yasiyo ya heshima

Maana inawezekana ni 1) 'kujitenganisha mwenyewe kutoka kwa watu wasioheshimika" au 2) 'anayejifanya safi.'

chombo cha hesima

Muhimu kwa ajili ya hafla maarumu" au " muhimu kwa ajili ya shughuli watu wema kufanya kwa wazi"

Maelezo ya jumla

Kama vile chombo chenye thamani kinavyoweza kutumika kwa njia za heshima katika nyumba yenye utajiri, mtu yeyote atakayemrudia Mungu atatumika kwa heshima katika kufanya kazi njema.

Ametengwa maalumu, mwenye manufaa kwa Bwana, na ameandaliwa kwa kila kazi njema.

"Bwana amemtenga na yupo tayari kutumiwa na Bwana kufanya kazi njema.

Ametengwa

Hajatengwa kimwili lakini katika kutimiza kusudi.

2 Timothy 2:22

Kimbieni tamaa za ujana

Mafumbo haya yanamaanisha mbio haraka uwezavyo. Kukimbia ni kukimbia kitu kitakachoweza kuwadhuru ninyi, kufuata ni kukimbia kuelekea kitu ambacho kitakufanyia mema.

ukafuate haki

"kuitafuta haki"

Na

Maana inawezekana ni 1) Paulo alimtaka Timotheo kujiunga na wakristo wengine katika kutafuta haki' au 2) Paulo alimtaka Timotheo awe na amani na sio kugombana na waamini wengine.

nao wamwitao Bwana

"Wakristo" au "wote ambao wanaojiita watu wa Mungu"

kwa moyo safi

"Kwa nia ya dhati" au "kwa sababu nzuri"

ukatae upumbavu na maswali ya kipuuzi

"Kukataa kujibu maswali ya upumbavu" na "maswali ya kipuuzi"

Moyo safi

Paulo anazungumza juu ya sababu nzuri za kufanya jambo toka moyoni.

Huzaa ugonvi

Paulo anazungumza juu ya maswali ya kipuuzi akiyafananisha na mwanamke anayezaa mtoto. "inasababisha ugonvi"

2 Timothy 2:24

katika upole

"Kondoo" au "upole"

elimisha

"Elekeza" au "mafundisho" au "kurekebisha"

kuwapatia toba

"Kuwasaidia kuiacha dhambi yao"

kwa ujuzi wa ile kweli

"Ili waweze kuujua ukweli"

wanaweza kurejesha fahamu zao"

"wanaweza tena kufikiri mawazo mabaya" au "wanaweza kuanza kusikiliza Mungu tena"

mtego wa Shetani

Hii ni mfano kwa ajili ya watu ambao wanadhani wao ni kufuatia Mungu wakati wao ni kweli zifuatazo shetani.

wametekwa na yeye kwa ajili ya mapenzi yake

"Ambaye aliwateka wao na sasa amewafanya kufanya chochote anachotaka wafanye'

2 Timothy 3

2 Timotheo 03 Maelezo kwa jumla

Muundo na Mpangilio

"Siku za mwisho" inaweza kuwa na maana ya hapo mbeleni kabla ya Kristo kurudi. Kwa hivyo Paulo anatabiri katika mistari 1-9 na 13 kuhusu siku hizo. "Siku za mwisho" pia inaeza maanisha kipindi cha Ukristo (pamoja na wakati wa Paulo).Kwa hivyo anayofundisha Paulo kuhusu mateso yanahusu Wakristo wote. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#prophet and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lastday)

<< | >>

2 Timothy 3:1

Sentensi Unganishi.

Paulo anataka Timotheo ajue ya kuwa katika siku za mwisho watu wataikataa kweri na mateso yatakuja, lakini katika hayo anaweza akalitumaini na kulitegemea andiko takatifu la Mungu.

Nyakati za Hatari.

Hizi zitakuwa ni siku, miezi na hata miaka ambayo Wakristo watakuwa katika hatari.

Wenye kujipenda wenyewe.

Matumizi ya neno "wenyekujipenda" inamaanisha upendo wa kiundugu au upendo wakiurafiki au watu wa familia moja, upendo wa asili kati ya marafiki na Jamaa(ndugu zao). Huu sio ya upendo utokao kwa Mungu.

Wenye majivuno.

Mtu yeyote mwenye kujisemea yeye katika hali ya kujisifu.

Wasiokuwa na Moyo wa kupenda.

"Wasiowapenda wa kwao( familia zao)

Wasio suluhishika

"Wasiokubaliana na mtu yeyote" au " wasio penda kusihi kwa amani na mtu yeyote".

Wasingiziaji.

"Washitaki wa uongo"

Wakali(wenye hasira)

"Katili" au " Mkali" au "watakuwa wakifanya mambo ili kuwaumiza wengine".

Wasiopenda Mema.

" Wenye kuchukia Mema"

Wakaidi.

"asiejali"( mtu wa kijiendea)

Majivuno( wenye viburi)

"Wakifikiri kuwa wao ni bora zaidi kuliko"

Siku za mwisho

Hii inamaanisha kuwa "anazungumzia siku za mbeleni baada ya Nyakati za Paulo. "Baadae kabla ya kurudi kwa Yesu"

2 Timothy 3:5

kuwa kama wacha Mungu

"Onekana kama wapenda dini au onekana kama wenye haki" au "Onekana kama watu wema"

Wataikana nguvu yake.

" Inamaana ya kuwa 1) "Wataikataa na wala hawataikubali nguvu ambayo Mungu alitaka kuwapatia" au 2) " Maisha yao hayataonesha udhibitisho wa ki Mungu kama wanavyodai".

Kutoka kwenye welekeo sahihi

" Kuepuka"

Watakao ingia kwenye familia

"Wakiingi katika nyumba na kushawishi sana"

Wanawake wapumbavu

"Wanawake ambao ni wachanga kiroho". Hii inaweza kuwa kwa sababu wanashidwa kutulia au kwa sababu hawana kazi au kwa sababu wamejawa na dhambi".

Waliojawa na dhaambi.

Maana zake ni 1) " Waliojawa na mizgo ya dhambi" au 2) " wanaotenda dhambi kila mara". Dhana kuu au wazo ni kwamba, hawawezi kuepukana na kutenda dhambi.

Wanaoongozwa na tamaa za kila aina.

Wanawake hawa hutamani vitu vingi kana kwamba wanaacha kumwabudu Kristo" au " Wanawake hawa wanaacha kumwabudu Kristo na badala yake wanaviendea vitu vingine wavitamanivyo."

2 Timothy 3:8

Yanne na Yambre

Majina haya mawili yanapatikana kwenye Biblia tu. Moja ya Mila inawaita kama waganga wa Misri waliokuwa wakimpinga Musa katika kitabu cha Kutoka 7-8.

Walisimama Kinyume

" Kupinga"

Sentensi unganishi

Paulo anawapa mfano wa walimu wawili wa uongo toka nyakati za Musa na kuonyesha namna watu watakavyokuwa. Anamsisitiza Timotheo kufuata mfano wa Paulo na kukaa katika neno la Mungu.

wako kinyume na kweli

"wanapinga injili ya Yesu"

Wamepotoka akili zao

"Hawawezi kufikiri kwa usahihi tena"

Kuendelea

" Kusonga mbele/ kupiga hatua"

Upumbavu

"Kutokuwa na uelewa" au " Upuuzi"

Dhahiri

"kuonekana wazi" au "kueleweka wazi"

Wasiokubalika kutokana na imani

Wanajaribiwa ni kwa namna gani wanamwamini Kristo na kumtii yeye na wakashindwa jaribu hilo. "bila imani ya kweli" au "wamethibitisha kuwa imani yao sio thabiti"

2 Timothy 3:10

wewe umeyafuata mafundisho yangu

" Lakini kwa wewe umekuwa makini katika kuyaangalia/kuyaenenda."

Mafundisho

"Maelekezo"

Mwenendo mzuri.

" Namna ya maisha"

Mateso ya mda

"kuwa na uvumilivu na watu"

Uvumulivu

Maana zake ni 1) "Nitaendelea kumtumikia Mungu hata katika hali ngumu ya kutoweza" au 2) " Nitaendelea kuenenda katika njia ya haki hata katika nyakati ngumu."

Walaghai/Watapeli

"Watu ambao huwadanganya watu kuhusu wao wenyewe" au " Watu ambao hujiweka tofauti na uhalisia wa maisha yao ya kweli."

Na katika hayo yote Bwana akaniokoa

Paulo anazungumzia namna ambavyo Bwana alimuokoa alipokuwa anateseka na hali ngumu na hatari.

kuishi katika maisha ya kumcha Mungu katika Kristo Yesu

"kuishi maisha ya kumcha Mungu kama mfuasi wa Yesu"

watateswa

"yawapaswa kuvumilia mateso"

watazidi kuwa waovu zaidi

"watakuwa waovu zaidi"

Watawapotosha wengine

"Watawasababisha watu wasimtii Kristo"

Wao wenyewe wamepotoshwa.

"Na watu wengine wawasababisha wasimtii Kristo"

2 Timothy 3:14

Endelea katika mambo ambayo umejifunza

" Usisahau yale uliyojifunza"

Maandiko matakatifu yatakayoweza kukufanya mtu mwenye hekima.

"Neno la Mungu linakupa Hekima utayoitaka"

2 Timothy 3:16

Kila andiko limeandikwa kwa uwezo wa Mungu

"Mungu aliyanena Maandiko yote kwa roho yake" au " Kila andiko ni pumzi ya Mungu", na kutolewa na roho wa Mungu. Mungu aliwambia watu nini waandike.

Lafaa.

"yenye kutumika" au " yenye faida"

Kuonya.

"kuonesha makosa"

Kurekebisha

"Kusahihisha makosa"

Kufundisha.

"kuwa mwenye maadili" au "kuleta katika uwezo wa kufanya kitu.

Mwenye uwezo dhabiti.

"Kuwa kamili"

mtu wa Mungu

Hii inamaana ya mtu yeyote anayemwamini Mungu awe mwanaume au mwanamke.

2 Timothy 4

2 Timotheo 04 Maelezo kwa jumla

Muundo na mpangilio

"Napeana amri hii ya dhati"

Paulo anapeana mashauri ya kibinafsi kwa Timotheo

Dhana Muhimu katika Sura hii

Taji

Maandiko matakatifu yanatumia aina nyingi ya mataji kama mfano wa vitu vingi. Inaonekana Kristo atawatuza waumini wake kama taji la kuishi maisha mazuri

__<< | __

2 Timothy 4:1

Sentensi unganishi.

Paulo aliendelea kumkumbusha Timotheo awe mwaminifu na kwamba Paulo yuko tayari kufa

Agizo lenye uzito

"Agizo la muhimu"

Mbele za Mungu na ya Kristo Yesu

"katika uwepo wa Mungu na Kristo Yesu"

walio hai na wafu

"walio hai na wafu" imetumika hapa kuwaelezea watu wote. "Watu wote waliowai kuishi"

kwa sababu ya kufunuliwa kwake na Ufalme wake

"Ufalme" inasimama kuonesha utawala wa Kristo kama Mfalme. "Atakaporejea kutawala kama mfalme"

Neno

"Neno" linamaanisha ujumbe. "Ujumbe kuhusu Kristo"

Usiofaa

"muda usiofaa"

Waambie watu dhambi zao

Kuwaambia watu makosa yao" au "kuwaambia watu kuwa walichofanya ni makosa"

himiza, kwa uvumilivu wote na mafundisho

"himiza na kufundisha watu na kuwa mvumilivu juu yao"

2 Timothy 4:3

kwa maana wakati unakuja

"kwasababu kwa muda fulani baadaya"

watu

Hali inaonyesha kuwa wale walikuwa watu wa kanisani

hawatachukuliana na mafundisho ya kweli

Hii ina maana kwamba mafundisho ambayo kanisa zima kuchukulia kuwa kweli na sahihi.

watajitafutia waalimu wa kufundisha kile wanacho kitamani, masikio yao yatakuwa tayari kusikia kile wakipendacho.

Maana inawezekana ikawa ni 1) kwa sababu ya tamaa zao binafsi, wao watajikusanyia karibu walimu ambao watasema nini wanataka kusikia au 2) kukusanya karibu walimu ambao wanakubaliana na tamaa zao binafsi na watasema nini wanataka kusikia.

masikio yao yatakuwa yametekenywa

Hii inamaanisha kuwa watu watafurahia kusikiliza mafundisho mapya na ya tofauti. "Kwa namna hii watatafta mambo mapya na ya tofauti ya kujifunza"

Wataacha kusikiliza mafundisho ya kweli

Paulo anazungumzia watu ambao hawajali tena na wala hawasikii. "hawasikilizi tena ukweli"

kazi ya uinjilisti

Hii ina maana kuwaambia watu kuhusu Yesu ni nani?alifanya nini kwaajili yao? na ni kwa jinsi gani waishi kwa ajili yake?

Watageukia hadithi

Paulo anazungumza na watu ambao wameanza kusikiliza hadithi. "wataanza kusikiliza hadithi ambazo si za kweli"

uwe mwaminifu

Paulo anataka wasikilizaji wake kuwa na fikra sahihi kwa kila jambo na aliwaambia wakitaka kuwa waaminifu wasitumie kileo.

2 Timothy 4:6

muda wa kuondoka kwangu umewadia

"Karibuni nitakufa na kuiacha dunia hii", Paulo alitambua kuwa hataishi kwa muda mrefu.

Nimeshindana katika mashindano mema

Hii ni michezo mfano wa mapigano, kumenyana, au ndondi. Paul amefanya kwa nguvu zake zote. Hii pia inaweza kutafsiriwa kama "Nimefanya kwa uwezo wote" au "Nilijitoa kwa nguvu zangu zote."

mwendo nimeumaliza

Picha hii inaashiria kumaliza maisha kama kufikia mstari wa kumalizia mbio. "Mimi nimemalize kile ninachohitajika kufanya."

imani nimeilinda

Maana inawezekana ikawa ni 1) "niimezishika mafundisho kuhusu nini tunaamini mbali na kila aina ya upotofu" au 2) "Nimekuwa mwaminifu katika kufanya huduma yangu"

Taji ya haki imewekwa kwa ajili yangu

"nitapewa taji ya haki'

Taji ya haki

Maana inaweze kuwa i 1) taji ni tuzo ambayo Mungu huwapa watu ambao wamekuwa wakiishi kwa njia sahihi au 2) taji ni mfano kwa ajili ya haki. Kama ambavyo hakimu wa mbio inatoa taji kwa mshindi, Paulo atakapomaliza maisha yake, Mungu atamtangaza kwamba Paulo ni mwenye haki.

taji

ni shada iliyotengenezwa kwa majani ya mti (laurel) ambayo ilitolewa kwa washindi wa mashindano ya riadha

siku ile

"siku ambayo Bwana atarudi tena" au "kwa siku ile Mungu atakapo wahukumu watu"

tayari nimekwisha kumiminwa

Paulo anazungumzia utayari wake wa kufa akijifananisha na kikombe cha mvinyo kilivyo tayari kumiminwa kama sadaka kwa Mungu.

bali pia kwa wote wanaongojea kwa shauku kuonekana kwake.

Hii inaweza kuelezewa kama tukio la wakati ujao. "lakini pia atawapa wale wangojao kwa shauku kurudi kwake"

2 Timothy 4:9

Sentensi unganishi

Katika kufunga kwake, Paul alimtia moyo Timotheo aje kwake, anamuambia amlete Luka, anataja baadhi ya watu ambao wamejitenga na Bwana, na anatoa salamu kwa wenyeji wa pale pamoja na Timotheo.

kwa haraka

"mapema iwezekanavyo"

kwani

kwasababu

dunia ya sasa

Maana inaweze ikana ni 1) mambo ya muda ya dunia hii, "raha na faraja ya dunia hii," au 2) hii maisha ya sasa na salama kutokana na kufa. Huenda Dema alikuwa na hofu kwamba watu wangeweza kumuua kama atakaa pamoja na Paulo.

Kreske alikwenda ......na Tito alikwenda

Watu hawa wawili waliondoka na kumuacha Paul, lakini Paulo hasemi kwamba wao pia "waliupenda ulimwengu huu wa sasa" kama Dema.

Dema ... Kreseni ... Tito

Haya ni majina ya wanaume.

Dalmatia.

Hili ni jina la mkoa

2 Timothy 4:11

yeye ni muhimu kwangu katika kazi hii

Maana inaweza ikawa ni 1) "anaweza kunisaidia katika huduma" au 2) "anaweza kunisaidia kwa kunihudumia mimi".

joho

Vazi zito linalovaliwa juu ya nguo

Karpo

Hili ni jina la mwanaume.

Vitabu

Hii inamaanisha "gombo" Hii ni aina ya kitabu kinachoandikwa kwenye ngozi. Baada ya kuandika au kusoma gombo hukunjwa kwa kutumia fimbo mwishoni.

Gombo dogo

Hii ni aina ya gombo. Hizi huwa zinatengenezwa kwa kutumia ngozi za wanyama"

2 Timothy 4:14

alinitendea maovu mengi

"alitenda maovu dhizi yangu" au "alinitendea mambo mabaya "

Bwana atamlipa kulingana na matendo yake

"Bwana atamuadhibu kutokana na aliyoyafanya"

yeye, yake

Yote haya yanamaanisha Alexanda

yeye alilipinga sana line neno letu

"Alipinga kwa jitihada kubwa ujumbe wetu" au "yeye alipinga sana maneno yetu"

hakuna mtu yeyote aliyesimama nami, badala yake wote waliniacha

"hakuna aliyekaa na mimi na kunisaidia, badala yake , kila mmoja aliondoka"

Tendo hilo lisihesabiwe dhidi yao

"mimi sitaki Mungu awaadhibu wale waumini kwa kuniacha mimi"

Alekizanda

Hili ni jina la mwanaume.

Mfua vyuma

"anayefanya kazi ya kutengeneza vyuma"

2 Timothy 4:17

alisimama pamoja nami

"alisimama pamoja nami kunisaidia mimi"

neno linenwe kwa ukamilifu na mataifa wapate kusikia

Maana inaweze kuwa ni 1) hii ilikuwa tayari kimeshatokea au 2) hii ilikuwa bado katika siku zijazo kwa ajili ya Paulo, "ili niweze kusema neno lake kikamilifu na hivyo watu wa mataifa yote wapate kusikia."

Niliokolewa katika kinywa cha simba

Hatari hii inaweza kuwa ni ya kimwili, kiroho, au vyote viwili. Mimi niliokolewa kutoka hatari kubwa."

2 Timothy 4:19

nyumba ya Onesiforo

"nyumba" inasimama kuelezea watu wanaoishi pale. "familia ya Onesiforo"

Onesiforo

Hili ni jina la mwanaume.

Erasto, Trifimo, Eubulo, Pude, Lino

Haya ni majina ya wamaume.

Mileto

Hili ni jina la mji uliopo kusini kwa Efeso.

Fanya hima uje

"tengeneza njia uje"

kabla ya kipindi cha baridi

"kabla ya kipindi cha baridi"

Pude, Lino, Claudia na ndugu wote

"Pude, Lino, Claudia na ndugu wote wanawasalimia"

Claudia

Hili ni jina la mwanamke.

Ndugu wote

"ndugu" inmaanisha waamini wote wanaume na wanawake.

Mungu awe pamoja na roho yako

"Naomba kwamba Mungu aifanye roho yako kuwa imara"

Neema iwe nanyi

"Naomba kwamba Bwana aoneshe rehema zake kwenu"

Neema

"huruma yake" au "upendeleo wake"

Utangulizi wa Tito

Utangulizi wa Jumla

Muhtasari wa kitabu cha Tito

  1. Paulo anamshauri Tito kuwateua viongozi wanaomcha Mungu (1:1-16)
  2. Paulo anamshauri Tito kuwafundisha watu kuishi maisha ya kumcha Mungu (2:1-3:11)
  3. Paulo anamalizia kwa kuelezea baadhi ya mipango yake na kutuma salamu kwa waumini. (3:12-15)

Nani aliandika kitabu chaTito?

Paulo aliandika Kitabu cha Tito. Hapo awali alijulikana kama Saulo. Alitokea mji wa Tarso. Kabla ya kuwa Mkristo alikuwa Mfarisayo na alikuwa akiwatesa sana Wakristo. Baada ya kuwa Mkristo, alisafiri mara nyingi katika himaya nzima ya Warumi akiwahubiria watu kumhusu Yesu

Kitabu cha Tito kinahusu nini?

Paulo alimwandikia barua hii Tito, mfanyakazi mwenza aliyekuwa anayaongoza makanisa ya Kisiwa cha Krete.Paulo alimwelekeza jinsi ya kuwachagua viongozi wa kanisa.Paulo pia alifafanua jinsi waumini walipaswa kutendeana.Na akawahimiza wote waishi maisha yanayompendeza Mungu.

Kichwa cha kitabu hiki kinafaa kitafsiriwe vipi?

Watafsiri wanaweza kukiita kitabu hiki kutumia kichwa chake cha kitamaduni, "Tito" ama wanaweza kuchagua kichwa kinachoeleweka zaidi kama, "Barua ya Paulo kwa Tito," ama "Barua kwa Tito." (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-names)

Sehemu ya 2: Dhana muhimu za kidini na kitamaduni

Watu wanaweza tumikia kanisa katika majukumu gani?

Kuna mafundisho fulani katika kitabu cha Tito kuhusu iwapo mwanamke ama mwanamume waliopeana talaka wanaweza kutumikia katika nafasi za uongozi kwenye kanisa. Wasomi wanatofautiana kuhusu maana ya mafundisho haya.Mafundisho zaidi kuhusu haya mambo yatakuwa ya muhimu kabla ya kukitafsiri kitabu hiki.

Sehemu ya 3: Maswala muhimu ya tafsiri

Umoja na wingi wa "wewe" na "ninyi"

Katika kitabu hiki, neno "mimi" linaashiria Paulo. Mara nyingi neno "wewe" inaashiria mtu moja, ndiye Tito, isipokuwa katika 3:15. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-exclusive and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-you)

Ni nini maana ya "Mungu mkombozi wetu"?

Hili ni tamko la kawaida katika barua hii. Paulo alitaka wasomaji wafikirie jinsi Mungu aliwasamehe kupitia kwa Kristo baada ya hao kumtendea dhambi. Na kwa kuwasamehe aliwaokoa kutoka kuadhibiwa wakati atakapowahukumu watu wote. Tamko sawa na hili katika barua hii ni, "Mungu wetu mkuu na Mkombozi Yesu Kristo."

Titus 1

Tito 01 Maelezo kwa jumla

Muundo na Mpangilio

Paulo anaanzisha barua hii kirasmi katika mistari 1-4. Waandishi walianzisha barua kwa njia hii hapo kale Mashariki ya Karibu.

Katika mistari ya 6-9, Paulo anaorodhesha sifa za mwanaume anayetaka kuwa mzee wa Kanisa. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-abstractnouns) Pauo anapeana orodha sawa katika 1 Timotheo 3.

Dhana muhimu katika sura hii

Wazee

Kanisa limetumia vyeo tofauti kuashiria viongozi wa kanisa. Baadhi ya vyeo hivi ni: Mwangalizi, mzee, mchungaji na askofu.

Maswala mengine tata katika tafsiri ya sura hii

Wanapaswa, wanaweza, Inawalazimu

ULB hutumia maneno tofauti kuwashiria mahitaji ama mambo ya lazima. Maneno hayo yana matumizi ya viwango tofauti vya misisitizo. Tofauti ndogo ya maana ya hayo maneno inaweza kuwa ngumu kutafsiri. UDB inatafsiri maneno hayo kwa njia ya jumla.

| >>

Titus 1:1

kwa imani ya

kuimarisha imani ya

inayokubaliana na utauwa

"inayofaa katika kumheshimu Mungu"

tangu milele (kabla ya nyakati zote)

"Kabla ya kuanza kwa wakati"

Katika wakati muafaka

"katika wakati unafaa"'

alilifunua neno

Paulo anaongea juu ya ujumbe wa Mungu kana kwamba ni kitu ambacho chaweza kudhihirishwa dhahiri kwa watu. "Alitangaza neno lake."

aliniamini mimi kuufikisha

"Niliaminiwa kutangaza" au "alinipa wajibu wa kuhubiri"

Mungu mwokozi wetu

"Mungu anayetuokoa"

Titus 1:4

Mwana wa kweli

Ingawa Tito hakuwa mwana wa Paulo kimwili, wanashiriki imani moja katika Kristo. Hivyo katika Kristo, Paulo humwona Tito kama mtoto wake. "wewe ni kama mwanangu"

Imani yetu ya kawaida

Paulo anaelezea imani ile ile ambayo wote wanayoshiriki katika Kristo. "Mafundisho yale yale ambayo sisi sote tunaamini"

Neema,huruma na amani

Hii ilikuwa salamu ya kawaida. "Neema,huruma na amani ziwe kwenu" au "mjazwe wema, huruma na amanikwenu."

Yesu Kristo mwokozi wetu

"Yesu Kristo ambaye ni mwokozi wetu"

Kwa kusudi hili

"Hii ni sababu"

Nilikuacha Krete

"Nilikuambia kubaki Krete"

Kwamba uyatengeneze mambo ambayo hayajakamilika

"Ili kwamba ungeamalizia kupanga mambo yaliyohitajika kukamilishwa."

Kuweka wazee

"chagua wazee" au "panga na kudhirisha wazee"

wazee

Katika makanisa ya kwanzaya Kikristo ,Wazee wakikristo walipewa uongozi wa kiroho kwa mkutano wa waumini.

Titus 1:6

Sentensi unganishi

Baada ya kuwa amekwisha kumwambia Tito kuwaweka kazini wazee katika kila mji katika kisiwa cha Krete, Paulo anatoa matakwa yanayohitajika kwa wazee.

Mzee lazima asiwe na lawama

Kutokulaumiwa ni ilie hali ya kujulikana kuwa mtu huyo hatendi mambo mabaya. "Mzee lazima asiwe na sifa mbaya."

Mme wa mke mmoja

"kuwa mme mwaminifu" Maana zinazokubalika 1) Mme ambaye hatafuti mahusiano na wanawake wengine au 2) asiye na mke wa pila au hawala au suria.

Watoto waaminifu

Imaana zinazokubalika ni 1)watoto wanaomwaminiYesu au 2)watoto ambao ni waaminifu

wasio na nidhamu

"waasi" au "ambao hawafuati maagizo"

msimamizi wa nyumba ya Mungu

Paulo anaongelea juu ya wazee kana kwamba walikuwa vichwa vya familia, wakuu wa nyumba ya Mungu"

Asiye...zoelea pombe

"asiwe mtu mwenye kutumia kileo" au "asiwe mnywaji" au "asiwe mlevi sana wa pombe"

Asiwe mgomvi

"Asiwe mtu wa fujo"au "asiwe anapenda kupigana na kugombana"

Titus 1:8

Badala

Paulo anabadili hoja kutoka mada inayohusu mambo yasimpasa mzee kwenda kwa mambo anayopaswa kufanya

Rafiki wa wema

"kukumbatia mambo mazuri na tabia nzuri"

kusimamia (kushikilia kwa nguvu)

Paulo anazungumzia hali ya kujitoa katika imani ya Kikristo kama kushikilia imani katika mikono. "kujitoa kwa " au " kuwa na ufahamu mzuri wa.."

Mafundisho mazuri

Lazima afundishe iliyo kweli kuhusu Mungu na mambo mengine ya kiroho.

Titus 1:10

sentensi unganishi

Kwa sababu ya wale wanaopinga neno la Mungu, Paulo anampa Tito sababu za kufundisha Neno la Mungu na kumwonya kuhusu waalimu wa uongo.

watu waasi

Hawa ni watu waasi waliokuwa wakiupinga ujumbe wa injili ya Paulo.

Wale wa tohara

inarejea wakristo wa Kiyahudi walikuwa wakifundisha kwamba ili kumfuata Kristo, mtu lazima atahiriwe.

Maneno yao ni upuuzi

'Maneno yao hayana faida yoyote"

Ni muhimu kuwakataza

"Ni lazima kuwazuia wasieneze mafundisho yao" au "Ni lazima kuwakataza kwa ushawishi wa maneno yao"

yale wasiyotakiwa kufundisha

Vitu ambavyo si sahihi kuvifundisha kuhusu Kristo na sheria.

Kwa faida ya aibu

"Hii inarejela faida ambayo watu wanapata kwa kufanya mambo yasiyo na heshima.

Wanaharibu nyumba nzima

"huharibu imani za familia yote"

Titus 1:12

Mmoja wao

"Mmoja wa Wakrete" au mtu fulani kutoka kwa watu wa Krete

Mtu busara

Maana zinazokubalika ni 1) nabii au 2) "mshairi au mwana falsafa au 3) mwalimu

Wakrete wana uongo usio na mwisho

"Wakrete hudanganya kila wakati" Maneno haya yametiwa chumvi kuonesha tabia wa Wakrete ya kudanganya.

wabaya na mnyama wa hatari

Msemo huu unawalinganish Wakrete na hayawani au wanyama hatari.

Wavivu na walafi

Ni msemo unaoonesha watu wasiopenda kufanya kazi yoyote lakini wanakula sana.

kuwazuia kwa nguvu ( kuwarekebisha)

kwa hiyo waambie kwa ujasiri kwamba hawako sahihi (wamekosea)"

Kwamba wanaweza kuwa katika imani ya kweli

"Watakuwa na imani imara" au " kwamba imani yao itakuwa ya kweli"

Titus 1:14

Sentensi kiunganishi

Paulo anaendelea na maagizo yake kwa kumwelekeza Tito kile anachotakiwa kufundisha

Hadithi za Kiyahudi

Hii inaonyesha kwa mafundisho ya uongo ya Wayahudi

kurudisha nyuma ukweli

Paulo anaongelea ukweli kana kwamba ni kitu kilicho katika mwendo ambacho chaweza kurudishwa nyuma. "Kukataa ukweli"

Titus 1:15

Kwa wale walio safi, vyote ni safi.

Kila kitu ni safi kwa yule aliye safi ndani yake. " kila kitu anachofanya kitakuwa safi"

kwa wale walio safi

kwa wale walimpokea Mungu

Kwa wale waliochafuliwa na wasioamini, hakunakilicho safi

Paulo anaongelea watu wenye dhambi kana kwamba ni wachafu kimwili. "Yeyote aliiye najisi kimaadili na ambaye haamini hawezi kuwa safi."

wanamkana kwa matendo yao

"matendo yao yanaonesha kuwa hawamjui"

waovu (wanachukiza)

mbaya, ya kutia kinyaa au isiyofaa

Hawakuthibitishwa kwa tendo lolote jema

"hakuna mtu yeyote anayewatarajia kufanya kitu chochote kizuri"

Titus 2

Tito 02 Maelezo kwa jumla

Dhana muhimu katika sura hii

Majukumu ya kijinsia

Wasomi wanatofautiana kuhusu jinsi ya kuielewa aya hii katika muktadha wake wa kihistoria na kitamaduni. Wasomi wengine wanaamini kwamba wanaume na wanawake wako sawa kwa maswala yote. Wengine wanaamini Mungu aliwaumba wanaume na wanawake kutumikia majukumu ya kipekee katika kanisa na ndoa.Watafsiri wawe makini wasiathiriwe na jinsi wanavyoelewa swala hili wakati wa kutafsiri aya hii.

Utumwa

Katika sura hii, Paulo haandiki iwapo utumwa ni mzuri ama mbaya. Paulo anafundisha kwamba watumwa wawafanyie mabwana wao kazi kwa uaminifu. Anawafundisha waumini wote kumcha Mungu na kuishi vyema katika kila hali.

<< | >>

Titus 2:1

Sentensi unganishi:

Paulo anaendelea kumweleza Tito sababu za yeye kuhubiri Neno la Mungu, na jinsi ambavyo wazee, akina mama wazee, vijana, na watumwa au watumishi wanapaswa kuishi kama waamini.

Lakini wewe

Paulo anatofautisha "Lakini wewe Tito, kinyume na walimu wa uongo"

na maelekezo ya kuaminika

"mafundisho ya kweli" au "na mafundisho sahihi"

Kiasi

"akili tengefu" au " "inayojijithibiti binafsi"

yenye busara

"inayojithibiti binafsi" au "inayotawala tamaa"

sahihi

"yenye afya"

sahihi katika imani

"yenye afya katika imani" au "sahihi katika imani zao"

Sahihi...katika pendo

"na upendo wenye afya"

sahihi...katika uvumilivu

"imara" au "ya kudumu" au "isiyochoka"

Titus 2:3

vivyo hivyo

"kwa njia iyo hiyo." "Kama unavyowaelekeza wazee, waelekeze akina mama pia."

lazima daima wajioneshe wao wenyewe

"wanapawa kudhihirisha wao wenyewe kuwa" au "Lazima uishi kama..."

kusengenya

Neno hili linarejelea watu wale wanaowasema vibaya wenzao kwa mambo ya kweli au ya uongo.

watumwa wa pombe

Mtu ambaye anatabia ya kuhitaji kunywa pombe mara kwa mara hupenda kunywa pombe nyingi. Paulo anaongelea juu ya watu waliokubuu au kuzoelea ulevi kiasi cha kuwaita watumwa. "watumwa wa pombe"

kuwa wenye busara... wasafi

kuwa na mawazo sahihi au kufikiri vizuri

Titus 2:6

kwa namna iyo hiyo

Tito alitakiwa kuwafundisha wasichana kama alivyokuwa akiwafundisha wazee.

jiwekeni wenyewe

Jioneshe wewe mwenyewe kuwa

mfano katika kazi nzuri

kielelezo cha mtu yule anayefanya mambo sahihi na yenye kufaa.

ujumbe wenye afya

Paulo anaongelea juu ya mahubiri na mafundisho ya Tito kana kwamba ni mtu mwenye afya katika mwili wake.

ili kwamba yeyote apingaye aaibishwe

Hii inawakilisha hali ya kufikirika ya kwamba mtu yeyote atakayempinga Tito ataaibishwa kwa kufanya hivyo. Ilikuwa haizungumzii hali halisi iliyokuwepo dhahiri. Huenda lugha yako yaweza kkuwa na njia fulani ya kuelezea jambo hili.

Titus 2:9

mabwana zao

"mabwana zao wenyewe"

katika kila kitu

"katika kila hali" au "mara zote"

kuwafurahisha

"kuwafanya mabwana zao wafurahi" au "kuwaridhisha mabwana zao"

kuiba

kuwaibia vitu vidogo mabwana zao

kuonesha imani nzuri

"kudhihirisha kuwa wanaaminika kwa mabwana zao"

katika kila njia

"katika kila jambo wanalolifanya"

kupamba mafundisho yetu

Paulo anazungumzia mafundisho ya kikristo kana kwamba ni kitu ambacho chaweza kupambwa. "Yafanyeni mafundisho yetu ili yawavutie watu wengine"

Mungu mwokozi wetu

"Mungu wetu anayetuokoa"

Titus 2:11

Sentensi kiunganishi

Paulo anamtia moyo Tito kuutarajia ujio wa Yesu na kukumbuka mamlaka yake kupitia kwa Yesu.

neema ya Mungu imeonekana.....Inatufundisha

Paulo anaiongelea neema ya Mungu kama ni Mtu anayeenda kwa watu wengine na kuwafundisha jinsi ya kuishi maisha matakatifu.

inatufundisha kukataa mambo yasiyo ya kimungu na tamaa za kidunia

Inatufundisha tusimwasi Mungu

tamaa za kidunia

"Hizi ni tamaa kali kwa ajili ya vitu vya dunia hii" au "tamaa kwa ajili anasa"

katika wakati huu

"wakati bado tunaishi katika dunia hii" au " "muda huu"

tunatarajia kupokea

"Tunasubiri kupokea"

tumaini letu lenye baraka,

Paulo anamaanisha kwamba Mungu atakuja kwetu ambaye ndani yake tumeweka tumaini letu .

mwonekano wa utukufu wa Mungu wetu mkuu na Mwokozi wetu Yesu Kristo.

Paulo anaongelea juu ya utukufu wa Mungu kumaanisha kwamba Mungu mwenyewe atajidhihirisha.

Titus 2:14

alijitoa mwenyewe

"kujitoa mwenyewe afe kwa ajili yetu."

kutukomboa kutoka katika uas

Paulo anamzungumzia Yesu aliyetukomboa kana kwamba anawaweka huru watumwa kutoka katika mikono ya mabwana zao waovu.

watu maalumu

Ni kundi la watu anaowawekezea hazina

walio na hamu

"kuwa na tamaa au hamu kubwa ya ajabu"

Titus 2:15

yaseme na kuyasisitiza mambo haya.

"Fundisha mambo haya na uwatie moyo wasikilizaji ili wayafanye mambo haya."

Kemea kwa mamlaka yote

Maelezo haya yanaweza kuwekwa wazi kama: " Wakemea au wasahihishe kwa mamlaka yote watu wale ambao hawayafanyi mambo haya"

Usikubali

"Usimruhusu mtu yeyote ku..."

akupuuze

Neno hili linnaweza kuwekwa wazi kumaanisha: " Kataa kusikiliza maneno yako" au "kukataa kukuheshimu"

Titus 3

Tito 03 Maelezo ya jumla

Muundo na Mpangilio

Paulo anampa Tito maelekezo ya kibinafsi katika sura hii.

Mstari wa 15 unamalizia barua hii kirasmi. Hii ni njia ya kawaida ya kumaliza barua siku za kale katika Mashariki ya Karibu.

Dhana muhimu katika sura hii

Orodha ya ukoo

Orodha ya ukoo no orodha inayorekodi mababu wa mtu. Wayahudi walitumia ordha za ukoo kumchagua mtu aliyestahili kuwa mfalme. Walifanya hivi kwa vile mwana wa kiume wa mfalme angekuwa mfalme. Zilionyesha pia ni kabila na familia gani walitokea. Kwa mfano makuhani walitoka katika kabila la Walawi na kwa familia ya Aruni.

__<< | __

Titus 3:1

Sentensi unganishi:

Paulo anaendelea kumpa Tito maelekezo juu ya namna ya kufundisha wazee na watu chini ya uangalizi wake huko Krete.

Uwakumbushe

"Kuwaambia watu wetu tena kile ambacho tayari wanakijua" au "Kuendelea kuwakumbusha"

nyenyekea kwa viongozi na mamlaka, kuwatii

"fanyeni kama watawala wa kisiasa na wenye mamlaka ya kiserikali wasemavyo kwa kuwatii"

watawala na wenye mamlaka

Maneno haya yana maana zinazofanana na yametumika pamoja kumuhusisha kila mmoja ambaye anashikilia mamlaka katika serikari.

muwe tayari kwa kila kazi njema

"muwe rayari kufanya mema wakati wote palipo na fursa"

ubaya

"ongea mabaya juu ya"

waache watu wengine waenende katika njia zao

Paulo anawasihi waumini kufanya mambo kama vile watu wengine wanavyopendelea kufanya, ilimradi tu matakwa yao na matendo yao yasiwe ya dhambi. "

Titus 3:3

kwa kuwa

"kwa sababu"

mwanzo

"zamani" au "kwa wakati fulani" au "awali"

mawazo potofu

"ujinga" au "kutokuwa na hekima"

potoshwa na kumikishwa kwa tamaa nyingi na starehe

Paulo anaongelea juu ya tamaa za dhambi kana kwamba ni watu wanaotupotosha kutoka katika njia ya kweli "tumepotoshwa"

tulifanywa watumwa kwa tamaa nyingi na starehe

Paulo anazizungumzia tamaa zetu mbaya za mwanzo na kuzifananisha na mabwana zetu waliotutumikisha.

shauku

"tamaa" au "hamu"

tuliishi katika uovu na wivu

"uovu na "wivu " ni maneno haya yako sawa kimaana, yaote yanamaanisha "dhambi." "Siku zote tulifanya mambo maovu na kutaka vitu vya watu wengine."

Tulichukiza

"tuliwafanya au tuliwasababisha wengine watuchukie"

Titus 3:4

wakati huruma wa Mungu mwokozi wetu na upendo wake kwa wanadamu ulipoonekana

Paulo anaongelea juu ya wema wa Mungu na Upendo wake kana kwamba walikuwa ni watu waliojitokeza mbele yetu.

kwa huruma yake

"Kwasababu alikuw na rehema juu yetu"

kutuosha kwa kuzaliwa upya

Paulo anazungumzia juu ya msamaha wa Mungu kwa wenye dhambi kwa kuufananisha na kitendo cha kuosha mwili wa mtu. Lakini pia, anaongelea juu ya wenye dhambi kuwa wasikivu mbele za Mungu kama wamezaliwa upya tena.

Titus 3:6

kwa utajiri

"kwa wingi" au "ukarimu"

alimwaga Roho Mtakatifu juu yetu

imekuwa kawaida kwa Waandishi wa Agano lake kumwongelea Roho Mtakatifu kama kimiminika ambacho humwagwa. "alitupa Roho Mtakatifu kwa ukarimu"

kupitia Mwokozi wetu Yesu Kristo

"Yesu alipotuokoa sisi"

tukiwa tumehesabiwa haki

"Mungu ametutangaza kuwa hatuna dhambi" "Tayari tumefanywa wenye haki na Mungu"

tulifanyika warithi katika uhakika wa maisha ya milele.

Watu walioahidiwa na Mungu waongelewa kama warithi wa mali na utajiri kutoka kwa mwana familia.

Titus 3:8

ujumbe huu

Hii inarejea kwenye maelezo kuhusu Mungu kutupa Roho Mtakatifu kupitia Yesu katika 3:6.

dhamira juu ya kazi nzuri

"kutafuta na kufanya matendo au kazi njema"

ambayo aliweka mbele yao

Paulo anaongelea kuhusu matendo meme kana kwamba ni vitu ambavyo Mungu aliweza kuviweka mbele ya watu. "ambayo Mungu aliyaandaa kwa ajili yao kuyafanya"

Titus 3:9

Sentensi unganishi:

Paulo anaelezea kile Tito anapaswa kuepuka na kuwashughulikia wale ambao wanasababisha ubishi miongoni mwa waumini.

Bali

"lakini wewe, Tito,"

mijadala ya kipumbavu

"mabishano kuhusu mambo yasiyo ya muhimu"

nasaba

mambo yanayohusu habari za uhusiano wa kifamilia au ukoo

ugomvi/mashindano

"kugombana"

sheria

"sheria za Musa"

Kataa/kumkataa

"kujitenga" au "kutoingiliana na" au "msikae na" au "kuepuka"

baada ya onyo moja au mawili

"baada ya kumuonya mtu huyo mara moja au mara mbili"

mtu wa aina hiyo

"mtu kama huyo"

ameiacha njia iliyo sahih

Paulo anamzungumzia mtu yule anayefanya makosa kana kwamba anaiacha njia ambayo amekuwa akiiendea.

anajilaani mwenyewe

"analeta hukumu juu yake mwenyewe"

Titus 3:12

Sentensi unganishi:

Paulo anafunga barua akimwambia Tito cha kufanya baada ya kuchagua viongozi katika Krete na kwa kumpa salamu kutoka kwa wale aliokuwa pamoja nao.

Nitakapo mtuma

"Baada ya kumtuma"

Artemi...Tikiko...Zena

Haya ni majina ya wanaume

harakisha na uje

"fanya haraka na uje" au "njoo haraka"

kukaa kipindi cha baridi

"kukaa wakati wa majira ya baridi"

Harakisha na umtume

"Harakisha" au "Usichelewe kutuma"

na Apolo

"na pia umtume Apolo"

Titus 3:14

Sentensi kiunganishi:

Paulo anafafanua kwanini ni muhimu wa kuwatoa akina Zena na Apolo.

watu wetu

Paulo alikuwa anawarejelea waumini wa Krete.

kujishughulisha wenyewe katika

"washughulike kufanya"

mahitaji muhimu

Haya ni mahitaji ya ambayo yalikuwa hayakupangwa na ya haraka ambayo yalikuwa hayajulikani hapo awali.

ili kwamba wasiweze kuwa wasiozaa matunda

Paulo anaongelea watu ambao hufanya matendo mazuri kama mimea inayozaa matunda ya kula. "ili waweze kuzaa matunda" au "ili maisha yao yawe na maana."

Titus 3:15

maelezo ya jumla

Paulo anahitimisha barua yake kwa Tito.

wote walio

"Watu wote"

wale watupendao katika imani

Maana zinazokubalika hapa ni 1) Waumini wanaotupenda au 2) Waumini wanaotupenda kwasababu tunashiriki imani moja.

Neema na iwe nanyi nyote

Hii ilikuwa ni salamu ya kawaida ya kikristo. "Neema ya Mungu na iwe pamoja nanyi" au "Ninamwomba Mungu awe mwenye neema kwenu ninyi nyote."

Utangulizi wa Filemoni

Sehemu ya 1: Utangulizi wa jumla

Muhtasari wa kitabu cha Filemoni

  1. Paulo anamsalimia Filemoni (1:1-3)
  2. Paulo anamuuliza Filemoni kumhusu Onesimo (1:4-21)
  3. Hitimisho (1:22-25)

Nani aliandika kitabu cha Filemoni?

Paulo alikiandika kitabu cha Filemoni. Hapo awali alijulikana kama Saulo. Alitokea mji wa Tarso. Kabla ya kuwa Mkristo alikuwa Mfarisayo na alikuwa akiwatesa sana Wakristo. Baada ya kuwa Mkristo, alisafiri mara nyingi katika himaya nzima ya Warumi akiwahubiria watu kumhusu Yesu

Paulo alikuwa gerezani alipoandika barua hii.

Kitabu cha Filemoni kinahusu nini?

Paulo aliandika barua hii kwa mwanaume aliyeitwa Filemoni. Filemoni alikuwa Mkristo aliyeishi katika jiji la Kolosae. Alikuwa na mtumwa aliyeitwa Onesimo. Onesimo alikuwa amemtoroka Filemoni na kuna uwezekano alikuwa pia amemuibia kitu.Onesimo alienda Roma na kumtembelea Paulo gerezani.

Paulo alimuambia Filemoni kwamba alikuwa anamtuma Onesimo kurudi kwake. Filemoni alikuwa na haki ya kumuua Onesimo kulingana na sheria za Warumi lakini Paulo akamsihi Filemoni kumkubali kama ndugu Mkiristo na akamshauri kumruhusu Onesimo kurudi kumsaidia Paulo gerezani

Kichwa cha kitabu hiki kinastahii kutasiriwa namna gani?

Watafsiri wanaweza kukiita hiki kitabu kutumia jina lake la kitamaduni, "Filemoni", ama wanaweza kuchagua kichwa kinachoeleweka wazi kama "Barua ya Paulo kwa Filemoni" ama "Barua Paulo alimwandikia Filemoni." (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-names)

Sehemu ya 2: Dhana muhimu za kidini na kitamaduni.

Je, barua hii inahalalisha utumwa?

Paulo alimtuma Onesimo kurudi kwa bwana wake. Hii haimaanishi kwamba alihalalisha utumwa. Paulo alizungumzia kuhusu watu kumtumkia Mungu katika hali zozote wangejipata ndani.

Paulo anamaanisha nini kwa maneno "ndani ya Kristo" na "Ndani ya Bwana"?

Paulo alitaka kuelezea wazo la kuwa na ushirika wa karibu sana kati ya muumini na Kristo. Tafadhali tazama utangulizi wa kitabu cha Warumi kwa maelezo zaidi kuhusu kauli hii.

Sehemu ya 3: Maswala muhimu ya tafsiri

Umoja na wingi wa "wewe" na "nyinyi"

Katika kitabu hiki, neno "mimi" linaashiria Paulo. Neno "wewe" linaashiria Filemoni isipokuwa katika sehemu mbili 1:22 na 1:25. Hapa "nyinyi" huashiria Filemoni na waumini waliokutana katika nyumba yake.Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-exclusive and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-you)

Philemon 1

Philemon 1:1

Paulo mfungwa wa Kristo Yesu, na Timotheo ndugu yetu kwa Filemoni

Lugha yako inaweza kuwa na njia maalum kwa mwandishi kujieleza kwa barua. "Sisi, Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu, na Timotheo, ndugu yetu, naandika hii barua kwa Filemoni."

mfungwa wa Kristo Yesu

"Mtu aliyefungwa kwa kufundisha kuhusu Yesu Kristo."

ndugu

Hapa hii inamaanisha mkristo mwenzake.

na mtendakazi mwenzetu

"Aliye, kama sisi, anakazi ya kueneza injili"

Afia dada yetu

Hii inamaanisha "Afia mkristo mwenzetu" au "Afia dada yetu kiroho"

Arkipo

Hili ni jina la mtu

Askari mwenzetu

Hapa ni "askari" ni fumbo inayomuelezea mtu anayepambana kwa kueneza injili. "Mwenzetu shujaa kiroho "au pia mpambanaji katika vita vya kiroho pamoja nasi."

neena iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo

"Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo awape neema na amani."Hii ni baraka. Neno "kwenu" ni kwa wengi na inarejea kwa watu wote waliosalimiwa na Paulo katika mstari wa 1 na 2.

Sentensi unganishi

Paulo amedhihirisha mara tatu kuwa yeye ni mwandishi wa barua hii. Timotheo alikuwa naye na aliandika maneno aliyoambiwa na Paulo. Paulo aliwasalimia waliokutana kusali katika nyumba ya Filemoni.

Maelezo ya jumla

Neno "mimi" linamaanisha Paulo. Filemoni ni mtu ambaye aliandikiwa barua hii. Sehemu zote zilizoandikwa "wewe" zinamuelezea Filemoni.

Maelezo ya jumla

Neno "yetu" inawajumuisha Paulo, Filemoni na waamini wa kanisa waliokuwa wakikutana kwenye nyumba ya Filemoni.

Baba yetu

Hiki ni cheo cha muhimu cha Mungu.

Philemon 1:4

Maelezo ya jumla

Neno "sisi" ni wingi ikimaanisha Paulo, Timotheo na Filemoni.

Wewe

Hapo na zaidi katika barua hii, neno" wewe" inamtaja Filemoni.

Kuwa na ufanisi katika ujuzi wa kila jambo jema

Matokeo ya kujua kilicho chema

Katika Kristo

"Kwa sababu ya Kristo"

mioyo ya waumini imekuwa ikitulizwa nawe

"umewatia moyo waamini" au "umewasaidia waamini"

Ndugu

"marafiki" Paulo anamuita Filemoni rafiki maana wote ni waamini na anasisitiza urafiki wao.

Philemon 1:8

Ujasiri wote katika Kristo

Inawezekana inamaanisha "mamlaka kwa sababu ya Kristo" au " kutiwa moyo kwa sababu ya Kristo."

lakini kwa sababu ya upendo

Inawezekana inamaanisha ni 1) "kwa sababu 1 ninajua unawapenda watu wa Mungu,"2) "kwa sababu unanipenda mimi" au 3) "kwa sababu ninakupenda."

Sentensi unganishi.

Paulo anaanza kutoa sababu ya kuandika barua yake.

Philemon 1:10

mwanangu Onesmo

"kijana wangu Onesmo." Paulo analinganisha uhusiano wake wa karibu na Onesmo sawa na ule uhusiano walionao baba na mwanawe. Kiuhalisia Onesmo sio kijana wa Paulo, lakini alipata maisha ya kiroho wakati Paulo alipomfundisha kuhusu Yesu, na Paulo alimpenda. "Mwanangu mpendwa Onesmo" au "Onesmo mwanangu wa kiroho."

Onesmo

Hili ni jina la mtu

niliyemzaa

Jinsi Onesmo alivyokuwa kama kijana kwa Paulo alimfanya kuwa muwazi. Niliyemfanya mwanangu wa kiroho wakati nilipomfundisha kuhusu Kristo na kuzaliwa mara ya pili." "amekuwa mwanangu"

katika vifungo vyangu

"katika minyororo. "Wafungwa mara nyingi kwa minyororo. Paulo alikuwa kifungoni wakati akimfundisha Timotheo, na aliendelea kuwa kifungoni hata wakati alipoandika barua hii. Wakati akiwa kifungoni."

Namtuma yeye ... kwenu

Paulo pengine ameandika barua kabla ya kumtuma Onesmo.

mpendwa wa moyo wangu.

Hapa neno "moyo" ilitumika kwa mtu anayependwa sana. Paulo alisema hivi kuhusu Oesmo. "Ambaye nampenda daima."

hivyo anaweza kunisaidia badala yako

"kwamba, tangu wewe usipokuwepo hapa, yeye ananguvu kunisaidia. Inaweza kutafsiriwa pia kama ni sentensi tofauti: Yeye angenisaidia mimi badala yako."

Mimi nimefungwa minyororo

"wakati nilipokuwa nimefungwa" au "kwa sababu nipo kifungoni."

kwa ajili ya injili

kwa sababu ya kuhubiri injili

Maelezo ya jumla

Onesmo alikuwa mtumwa na Filemoni aliyemuibia kila kitu na kukimbia.

Philemon 1:14

Lakini sikutaka kufanya jambo lolote bila ridhaa yako

"Lakini sikutakutaka kumweka yeye hapa bila idhini yako" au "Lakini nilitaka awe pamoja nami kama wewe umekubali"

hivyo kila jambo zuri ulilofanya si kwa sababu nimekulazimisha

hivyo kila jambo jema utakalofanya, si kwa sababu nakulazimisha."

lakini kwa sababu ulitaka kufanya

"kwa sababu uliwa huru kuchagua kufanya jambo lililo jema"

labda kwa sababu mlitengwa naye

Hii yaweza kutafsiriwa hivi "Labda ni sababu ya Mungu kumpeleka Onesmo awe mbali nawe."

kwa wakati

"kwa muda huu"

bora zaidi ya mtumwa

"ana thamani zaidi ya mtumwa"

ndugu mpendwa

"ndugu mpendwa" au "ndugu wa thamani katika Kristo"

zaidi sana kwako

"anamaanisha zaidi sana kwako"

kibinadamu

uhusiano wa kibinadamu unaweza kuonekana wazi: "kwa sababu yeye ni mtumwa wenu" "kama mtu" au "uhusiano wa kibinadamu."

na katika Bwana

"na kama ndugu katika Bwana" au na kwa sababu yeye ni mali ya Bwana."

Philemon 1:17

kama unanichukulia kama mshiriki

"kama wewe unanidhania mimi mtenda kazi wa Kristo"

unidai mimi malipo

"malipo yatatoka kwangu" au "sema kwamba mimi ni mmoja wa unaowadai."

mimi Paulo ninaandika kwa mkono wangu

Paulo niliyeandika hivyo, kwamba Filemoni ujue kwamba ni maneno ya kweli; Paulo kweli angemlipa. "Mimi, Paulo, ninaandika hivi mwenyewe."

Sikutaka kukwambia

"Sikuhitaji kukukumbusha wewe" "wewe unajua"

unanidai maisha yako

"wewe unanidai maisha yako" Paulo anamwambia Filemoni asiseme kuwa anawadai Onesmo au Paulo maisha yake kwa sababu Paulo anamdai zaidi Filemoni. "Ninakudai zaidi maana nimeyaokoa maisha yako"

furahisha moyo wangu

Paulo alitaka Onesmo angefanya kwa uaminifu: furahisha moyo wangu kwa kumkubali Onesmo. "uufanye moyo wangu ufurahi" au "unifurahishe" au "unifariji."

Philemon 1:21

Ujasiri kuhusu utii wako

"Kwa sababu nina hakika kwamba utafanya kile nilichosema"

Na wakati mwingine

"Pia"

andaa chumba kwa ajili yangu

andaa chumba hapo kwako iwe tayari kwa ajili yangu. Paulo alimwambia Filemoni afanye hivyo.

nitakutembelea hivi karibuni

"Wale walioniweka gerezani wataniachia huru hivyo ntakuja kwako"

Sentensi unganishi

Paulo anamalizia barua yake kwa kuwabariki Filemoni na waamini wote waliokuwa wakikusanyika kusali katika nyumba ya Filemoni.

Maelezo ya jumla

Maneno "wewe, ninyi" yanawaelezea Filemoni na waamini waliokutana nyumbani.

Philemon 1:23

Epafra

Huyu alikuwa mwaminu na mfungwa pamoja na Paulo.

mfungwa mwenzangu katika Kristo Yesu

"ambaye yupo gerezani pamoja na mimi kwa sababu ya Yesu Kristo"

Marko, Aristarko, Dema, Luka, watendakazi wenzangu.

Marko, Aristarko, Dema, Luka, watendakazi wenzangu nawasalimu.

Marko ... Aristarko ... Dema ... Luka

Haya ni majina ya watu.

watendakazi wenzangu

"wafanyakazi wenzangu" au "wote wanaofanya kazi na mimi"

Neema ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho yako.

Neno "yako" inawaelezea Filemoni na wote waliokutana nyumbani. "roho yako" inawakilisha watu wenyewe. "Bwana wetu Yesu Kristo awe mwema kwenu"

Utangulizi wa Waebrania

Sehemu ya 1: Utangulizi wa jumla

Muhtasari wa kitabu cha Waebrania

  1. Yesu ni mkuu kuliko manabii wa Mungu na malaika (1:1-4:13)
  2. Yesu ni mkuu kuliko makuhani wanaohudumu katika hekalu la Yerusalemu (4:14-7:28)
  3. Huduma ya Yesu ni kuu kuliko agano la kale Mungu alilofanya na watu wake (8:1-10:39)
  4. "Imani ni kama nini (11:1-40)
  5. Kutia moyo kuwa mwaminifu kwa Mungu (12:1-29)
  6. Mahimizo ya kumalizia na salamu (13:1-25)

Nani aliandika kitabu cha Waebrania?

Hakuna ajuaye mwandishi wa Waebrania. Wasomi wanapendekeza watu kadhaa ambao kuna uwezekano waliandika Waebrania. Watu hawa ni Paulo, Luka na Barnaba. Tarehe ya kukiandika pia hakijulikani. Wasomi wengi wanafikiri kiliandikwa miaka mbele ya mwaka wa 70 A.D..Yerusalemu iliharibiwa 70 A.D. lakini mwandishi wa kitabu hiki anazungumzia Yerusalemu kana kwamba ulikuwa bado haujaharibiwa.

Kitabu cha Waebrania kinahusu nini?

Katika kitabu cha Waebrania, mwandishi anaonyesha kwamba Yesu alitimiza unabii za Agano la Kale. Mwandishi alifanya hivi kuwahimiza Wakristo Wayahudi kwamba Kristu ni bora kuliko kitu chochote Agano la Kale lingepeana.Yesu ndiye Kuhani Mkuu bora. Yesu pia ndiye dhabihu bora. Dhabihu ya wanyama yalikosa maana kwa sababu dhabihu ya Yesu ilitolewa mara moja na ya mwisho. Kwa hivyo Yesu ndiye njia pekee ya watu kukubalika na Mungu.

Kichwa cha kitabu hiki kinastahili kutafsiriwa namna gani?

Watafsiri wanaweza kuamua kukiita kitabu hiki kutumia kichwa chake cha kitamaduni ,"Waebrania" ama wanaweza kuchagua kichwa kinachoeleweka zaidi kama "Barua kwa Waebrania" ama "Barua kwa Wakristo Wayahudi." (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-names)

Sehemu ya 2: Dhana muhimu za kidini na kitamaduni

Je, wasomaji wanaweza elewa kitabu hiki bila kufahamu kuhusu dhabihu na kazi ya makuhani katika Agano la Kale?

Itakuwa vigumu kwa wasomaji kuelewa kitabu hiki bila kuyaelewa maswala haya. Watafsiri wanaweza pendekeza kuzifafanua baadhi ya dhana hizi za Agano la Kale kwa maelezo ama katika utangulizi wa kitabu hiki.

Swala la damu limetumika vipi katika kitabu cha Waebrania?

Kuanzia Waebrania 9:7 swala la damu linatumika kuashiria kifo cha mnyama yeyote ambaye alitambikwa kulingana na agano la Mungu pamoja na Israeli. Mwandishi pia anatumia damu kuashiria kifo cha Yesu Kristo.Yesu alikuwa sadaka kamilifu ili Mungu awasamehe watu sababu walimtendea dhambi.(Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metonymy)

Kuanzia Waebrania 9:19, mwandishi anatumia swala la kunyunyuzia damu kama tendo la maana ya mfano. Katika Agano la Kale makuhani walinyunyuzia damu ya wanyama waliotolewa sadaka. Hii ilikuwa ni ishara ya faida za kifo cha mnyama kuelekezewa watu ama kitu. Hii ilimaanisha kwamba watu ama kitu kilikubalika/walikubalika kwa Mungu.(Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-symaction)

Sehemu ya 3: Maswala muhimu ya tafsiri.

Maswala ya "Takatifu" na "takaza/takatatifuzwa" yameasilishwa namna gani katika Waebrania kwa ULB?

Maandiko yanatumia maneno kama haya kuashiria maswala mbalimbali.Kwa sababu hiyo, mara nyingi ni vigumu kwa watafsiri kuyawakilisha vyema katika matoleo yao.Kuyatafsiri katika Kiingereza, ULB hutumia sheria zifuatavyo:

UDB itakuwa na usaidizi wakati watafsiri anafikiria jinsi ya kuwakilisha mawazo haya katika matoleo yao wenyewe.

Ni maswala gani muhimu katika maandishi ya kitabu cha Waebrania?

Katika mistari ifuatayo, matoleo ya kisasa ya Bibilia yanatofautiana na matoleo ya kale. ULB ina masomo ya kisasa na huweka masomo ya zamani kama maelezo ya chini. Kama kuna tafsiri ya Bibilia katika eneo jumla, watafsiri wanafaa kuzingatia kutumia masomo yaliyo kwenye hayo matoleo. Kama si hivyo, watafsiri wanashauriwa kutumia masomo ya kisasa.

(See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/jit.html#translate-textvariants)

Hebrews 1

Waebrania 01 Maelezo kwa jumla

Muundo na Mpangilio

Sura hii inaonyesha jinsi Yesu ni muhimu kwa sisi kuliko malaika.

Watafsiri wengine wametenga kila mshororo wa ushairi kulia kuliko maandishi mengine ili isomeke kwa urahisi. ULB inafanya hivi na ushairi katika 1:5, 7-13, ambayo ni maneno kutoka Agano la Kale.

"Mababu wetu"

Mwandishi aliandikia barua hii Wakristo waliokuwa wamekua kama Wayahudi.Hii ndiyo maana barua hii inaitwa "Waebrania".

Mifano muhimu ya hotuba

Maswali ya hadithi

Mwandishi anatumia maswali ya hadithi kama njia ya kuthibitsha kwamba Yesu ni bora kuliko malaika. Yeye pamoja na wasomaji wake wanafahamu majibu ya maswali na mwandishi anajua kwamba wakati wasomaji wanafikiria juu ya majibu ya maswali, watakuja kufahamu kwamba Mwana wa Mungu ni muhimu kuliko malaika wowote.

Ushairi

Walimu Wayahudi sawa na manabii wa Agano la kale, waliyaweka masomo yao mengi ya muhimu kwa ushairi ili wasikilizaji waelewe na kuyakumbuka.

| >>

Hebrews 1:1

Sentensi Unganishi:

Hii inaweka msingi wa kitabu chote: Ukuu wa Mwana- Mwana ni mkuu kuliko wote. Kitabu kinaanza na msisitizo kwamba Mwana ni mkuu kuliko manabii na malaika.

Maelezo ya Jumla:

Ingawa haijaelezwa mwanzoni mwa kitabu, barua hii iliandikwa kwa Waebrania Wakati (Wayahudi) ambao kimsingi walikuwa wanaelewa maelekezo mengi ya Agano la Kale.

Kupitia Mwana

''Mwana" ni cheo muhimu kwa Yesu, Mwana wa Mungu.

Mungu kuwa mrithi wa vitu vyote

Mwandishi anamwelezea kana kwamba Mwana atarithi utajiri na mali kutoka kwa Baba. AT: " kumilili vitu vyote"

Mungu aliuumba ulimwengu kupitia yeye

"Ni kupitia yeye pia Mungu aliviumba vitu vyote.

Mwana

Hiki ni cheo muhimu kwa Yesu, Mwana wa Mungu.

mng'ao wa utukufu wa Mungu

"mwanga wa utukufu wake.'Utukufu wa Mungu una muunganiko wa mng'ao sana. Mwandishi anasema Mwana anabeba mng'ao huo na anamwakilisha Mungu kwa ukamilifu.

tabia sawa ya asili yake

"sura ya Uungu wa mungu." Hii ina maana sawa na "mng'ao wa utukufu wa Mungu" Mwana anabeba tabia na asili ya Mungu na anawakilisha uungu wote wa Mungu. inaweza kusemwa katika

neno la nguvu zake

"neno lake la nguv." Hapa "neno" linamaanisha ujumbe au amri. AT: "amri yake ya nguvu"

Baada ya kufanya utakaso kwa ajili ya dhambi

Jina dhaniwa"takasa" linaweza kuelezea kama kitenzi: "kufanya safi." AT: "Baada ya kumaliza kutufanya kuwa safi' au baada ya kumaliza kututakasa kutoka katika dhambi zetu"

amefanya utakaso kwa ajili yetu

Mwandishi anaongea juu ya msamaha wa dhambi kana kwamba ulikuwa unamfanya mtu kuwa safi. AT: amefanya uwezekano kwa ajili ya Mungu kusamehe dhambi"

aliketi katika mkono wake wa kuume wa mwenye enzi"

Hapa "mkono wa kulia" linamaanisha sehemu ya utukufu.AT: "aliketi katika sehemu ya utukufu karibu na kwenye enzi"

Mwenye enzi aketiye juu

"Hapa "enzi" linamaanisha Mungu. AT: "Mungu mwenye enzi

Hebrews 1:4

maelezo ya Jumla:

Hii ni nukuu ya kinabii (Wewe mwanangu) inatoka katika Zaburi. Nabii Samweli aliandika unabii wa pili (nitakuwa baba kwake). Maneno yote ambaye yanamaanisha Yesu. Neno "Wewe" linamaana ya Yesu, na neno "Mimi" linamaanisha Mungu Baba.

Amekuwa

''Mwana amefanyika"

Kama jina alilorithi ni bora zaidi ya majina yao Kwa malaika gani aliwahi kusema ...baba"?

Mwanaidishi anaongea katika swala la kupokea heshima na mamlaka kana kwamba alikuwa akirithi utajiri na mali kutoka kw baba yake.AT: "amepokea."

Ni malaika wapi Mungu alimewahi kuwambia "Wewe ni mwanangu... mwana kwangu"?

Swali linasistiza kuwa Mungu hamwita malaika yeyote mwana wake. AT: " kwa sababu Mungu hajawahi kumwabia malaika yeyote 'Wewe ni mwana wangu... mwana kwangu."

Na tena...kwangu

"Na tena, hakuwahi kusema kwa malaika yeyote, '...kwangu'?"

Wewe ni mwanangu...nimekuwa baba yako...nitakuwa baba kwake...atakuwa mwana kwangu

Uhusiano maalumu Mungu Baba alionao na Mungu Mwana umeelezwa katika Agno la Kale mamia ya miaka kabla ya Yesu kuzaliwa.

Wewe ni mwanangu... nimekuwa baba yako

maneno haya kimsingi yanamaanisha kitu kimoja.

Hebrews 1:6

Maelezo ya Jumla:

Nukuu ya kwanza katika sehemu hii (Malaika wote wa Mungu...) inatoka katika moja ya kitabu alivyoandika Musa. Na nukuu ya pili (Yeye afanyaye ...) inatoka katika kitabu cha Zaburi.

Mzaliwa wa kwanza

Hii inamanisha Yesu.Mwandishi anamwelezea Yesu kama "mzaliwa wa kwanza" kusisitiza umuhimu na mamlaka juu ya mtu yeyote. Haina maana ya kuwa kulikuwa na wakati fulani ambao Yesu hakuwepo au kwamba Mungu alikuwa na wana kama Yesu. AT: "Mwana wake mheshimiwa, Mwana wake wa pekee.

akasema

"Mungu anasema"

Yeye awafanyaye malaika wake roho, na watumishi wake miali ya moto

Maana inayowezekana: 1) "Mungu amewafanya malaika wae kuwa roho zinazomtumikia kwa nguvu kama miali ya moto." (UDB) au 2)Mungu hufanya upepo na miali ya moto kuwa "watumwa" na watumishi wake. Katika lugha za asili neno "malaika" ni sawa na neno "mtumishi," na neno "roho" ni sawa na "upepo." Kwa maana yoyote ile ujumbe kusudiwa ni kwamba malaika wanamtumika Mwana kwa kuwa ni mkuu,

Hebrews 1:8

Maelezo ya Jumla:

Nukuu hii ya andiko inatoka katika kitabu cha Zaburi

Kuhusu Mwana anasema,

"Lakini Mungu asema hivi kuhusu Mwana"

Mwana

Hiki ni cheo muhimu kwa Yesu, Mwana wa Mungu.

Kiti chako cha enzi, Mungu ni cha milele

Kiti cha enzi kinawakilisha utawala. AT: " Wewe ni Mungun na utawala wako utadumu milele"

fimbo yako ya ufalme ni ya haki

Fimbo yautawala inamaanisha utawala wa Mwana. AT: "Na utatawala juu ya watu katika ufalme wako kwa haki"

amekupaka mafuta ya furaha zaidi ya wenzako

Hapa "mafuta ya furaha" inamaanisha furaha aliyokuwa nayo wakati Mungu alipo muheshimu. AT:"amekuheshimu na amekufanya kuwa na furaha zaidi ya yeyote.

Hebrews 1:10

Sentensi Unganishi:

Mwanadishi anaendelea kufanua kwamba Yesu ni mkuu kwa malaika.

Maelezo ya Jumla:

Nukuu hii inatoka katika Zaburi.

Hapo mwanzo

"Kabla ya kitu chochote hakijakiwapo"

uliweka misingi ya nchi

Mwandishi anaongea Mungu kuumba dunia kana kwamba anajenga juu ya msingi. AT: " uliumba dunia"

Mbingu ni kazi za mikono yako

Hapa "mikono" inamaanisha nguvu na matendo ya Mungu.AT: "uliziumba mbingu"

Zitaharibika

"Mbingu na nchi zitapotea" au " mbingu na nchi hazitakuwepo tena"

zitachakaa kama kipande cha nguo

Mwandishi anaongea juu mbingu na nchi kama ilikuwa ni kipande cha vazi ambayo itazeeka na mwishowe na kutofaa.

atazianua kama vazi

Mwandishi anaongea kana kwamba mbingu na na nchi ni nguo au aina nyingine ya vazi.

Vitabadilishwa kama kipande cha nguo

Mwandishi anaongea juu ya mbingu na na nchi kana kwamba ni nguo ambazo zinaweza kubadlishwa

zitabadilishwa

Hii inaweza kusema katika muundo tendaji. AT: "utazibadilisha"

Miaka yako haina mwisho

Vipindi vya nyakati vinatumika kuwakilisha Uwepo wa Mungu wa milele.AT: "maisha yako hayatakuwa na mwisho"

Hebrews 1:13

Maelezo ya Jumla

Nukuu hii inatoka katika Zaburi nyingine.

Lakini ni malaika gani wakati wowote Mungu amesema...miguu?

Mwandishi anatumia swali kusisitiza kwamba Mungu hajawahi kumwambia malaika. AT: '"Lakini Mungu hajamwambia malaika yeeyote wakati wowote"'

Keti mkono wangu wa kulia

Hapa mkono wa kulia unamaanisha sehemu ya heshima. AT: "Kaa karibu yangu katika sehemu ya heshima"

Hadi nitakapo waweka maadui wako chini ya miguu yako

Maadui wa Kristo wanaongelewa kana kwamba watakuwa chombo ambachomfalme anaweka miguu yake, Picha hii inawakilisha kushindwa na aibu kwa maadui wake.

Sio malaika wote ni roho... wanarithi wokovu

Mwandishi anatumia hili swali kuwakumbusah wasomaji wake kwamba malaika hawana nguvu kama Kristo, lakini wana jukumu tofauti. AT: "malakia wote ni roho ambazo... hurithi wokovu."

kwa wale watakaorithi wokovu

Kupokea kile ambacho Mungu amewaahidi waumini imeongelewa kana kwamba wanarithi utajiri na mali kutoka katika mwana familia. AT: "kwa ajili ya wale wote ambao Mungu atawaokoa"

Hebrews 2

Waebrania 02 Maelezo kwa jumla

Muundo na mpangilio

Sura hii inahusu jinsi Yesu ni bora kuliko Musa, Mwisraeli mkuu kuliko wote.

Watafsiri wengine wameweka kila msitari wa ushairi kulia kuliko maandishi mengine ili isomeke kwa urahisi. ULB inafanya hivi na ushairi katika 2:6-8, 12-13, ambayo ni maneno kutoka Agano la Kale.

Dhana muhimu katika sura hii

Ndugu

Huenda mwandishi anatumia neno "ndugu" kuashiria Wakristo waliokua kama Wayahudi.

<< | >>

Hebrews 2:1

Sentensi Unganishi:

Hili ni onyo la kwanza kati ya maonyo matano mwandishi anatoa

Ni lazima

Hapa "sisi"inamaanisha mwandishi anajijumuisha kwenye kundi lake.

ili kwamba tukatengwa/ kuchukuliwa mbali

kuamini katika neno la Mungu kidogo huongelewa kana kwamba mtumbwi ulikuwa ukichukuliwa mbali juu ya maji kutoka mahali ulipaswa kuwa. AT: " ili kwamba polepole tusiache kuliamini."

Hebrews 2:2

Kama ujumbe uliozungumzwa kupitia malaika

Wayahudi waliamini kuwa Mungu alisema sheria yake kupitia malaika. Hii inaweza kuelezewa katika mfumo tendaji. AT: "Kama ujumbe ambao Mungu aliongea kupitia malaika"

Kwa kuwa kama ujumbe

Mwandishi ana hakika kuwa mambo haya ni kweli. AT: "Kwa sababu ujumbe"

Ni halali

"ni sahihi au "kweli"

kila kosa na uasi hupokea adhabu ya haki

Neno kosa and uasi husimama kwa ajili ya watu ambao wana hatia kwa ajili ya dhambi hizi. AT: "kila mtu atendaye dhambi atapokea adhabu ya haki"

kosa na uasi

maneno haya mawili kimsingi yanamaanisha kitu kimoja.

tutapataje kuepuka kama tusipojali wokovu mku u kama huu?

Mwanadishi anatumia swali kusisitiza watu wata pokea adhabu kama watakataa wokovu wa Mungu kupitia Kristo. AT: "hivyo Mungu atatuadhibu kama hatuutilii manani ujumbe wake kuhusu vile Mungu atakavyo tuokoa!"

kutojali

"kutojali" au "kuona sio muhimu"

Huu ni waovu ambao kwanza ulitangazwa na Bwana

Hii inaweza kusemwa katika mtumo tendaji. AT: "Bwana mwenyewe kwanza alitangaza ujumbe vile atakavyo tuokoa"

na ametuthibitishia kupitia wale walio sikia

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. " na wale walio siki ujumbe walituthibitishia"

kulingana namapenzi yake

" kama jinsi alivyopenda kufanya"

Hebrews 2:5

Sentensi Unganishi:

Mwandishi anawakumbusha Waebrania hawa kwamba siku moja nchi itakuwa chini ya utawala wa Bwana Yesu.

Maelezo ya Jumla:

Nukuu hapa inatoka katika kitabu cha Zaburi katika Agano la Kale. Inaendele hadi sehemu inayofuata.

Kwa sababu kama haikuwa kwa malaika ambao Mungu aliwaweka

"Kwa kuwa Mungu hakuwaweka malaika kuwa watawala"

Ulimwengu ujao

"Ulimwengu" hapa unamaanisha kwa watu wanaoishi huko. Na "ujao" unamaanishi huu ni ulimwengu uajao baada ya Yesu atakaporudi. AT: "watu watakaoishi katika ulimwengu wa mpya"

Mtuni nani, kwamba uweze kumkumbuka/ kumjali?

Swali linatumika kusisitiza kuwa wanadamu sio muhimu kwa kumfanya Mungu kuwajal.AT: "Hakuna mwandamu ambaye ni wa Muhimu wa kumfanya Mungu kufikiri kuhusu yeye!"

Au mwana wa mtu , kwamba umjali?

Kimsingi hii inamaanisha kitu kilekile kinachoelezewa katika swali la kwanza. Swali lisilo hitaji kujibiwa linasisitiza mshangao kwamba wanadamu si wa muhimu kiasi cha kwamba Mungu awajalli.AT: "Hakuna mwanadamu anayesitahili kujaliwa na wewe!"

Hebrews 2:7

mdogo kuliko malaika

Mwandishi anamuongelea mwanadamu kuwa sio wa muhimu kuliko malaika kana kwamba wanadamuwamesimama katika nafasi amabayo ni ya chini kuliko nafasi ya malaika. AT: "mdogo kuliko malaika."

amemfanya mtu...amevika... miguu yake... kwake

Maneno haya sio kwa ajili ya mlengwa mmoja bali inajumuisha wanadamu wote, inajumuisha wanaume na wanawake.AT: "amewafanya wanadamu... amewavika...miguu yao... kwao"

umemvika utukufu na heshima

zawadi ya utukufu na heshima zinaongelewa kana kwamba ni shada la majani lililowekwa kichwani mwa mshindi wa mchezo. AT:"umewapa utukufu mwing na heshima"

Umeweka kila kitu kiwe chini ya miguu yake

Mwandishi anamuongelea mwanadamu kuwa na utawala juu ya kila kitu kana kwamba wamesimama juu ya kila kitu. AT: "Umewapa kumiliki juu ya vitu vyote"

Hakuacha kitu chochote kisicho kuwa chini yake

maneno mawili hasi yanamaanisha kwamba vitu vyote vitawekwa chini ya Kristo. AT: "Mungu alifanya kila kitu kuwa chini yao"

Hatuoni vitu vyote vikiwa chini yake

tunafahamu kuwa bado wanadamu hawajawa wamiliki wa kila kitu

Hebrews 2:9

Sentensi Unganishi:

Mwanadishi anawakumbusha hawa Webrania waumini kwamba Kristo alipokuaja duniania alifanyika mdogo kuliko malaika alipokuja dunia kuteseka kufa kwa ajili ya msamaha wa dhambi, na kwamba alifanyika kuhani mkuu mwenye huruma.

tunamwona ambaye

"twafahamu kuwa kuna mwingine"

aliyefanyika

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji.AT: "ambaye Mungu alimfanya'

chini kuliko malaika...amevikwa utukufu na heshima

Tasifri hii kama ulitafsiri sura ya 2:7

amevikwa

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: "Mungu alimvika'

amaeonja kifo

Uzoefu wa kifo unaongelewa kana kwamba kifo ni chakula kilichoonjwa.AT: "ameonja kifo" au "amekufa"

kwa kuwa kila mtu

"Mtu" hapa linamaanisha watu wote. wakijumuishwa wanaume na wanawake. AT: "kwa kuwa kila mtu"

awaleta wana wengi katika utukufu

Zawadi ya utukufu hapa inaongelewa kana kwamba ni sehemu ambayo watu wangeweza kuletwa. AT: "awaokoe wana wengi"

wana wengi

Hapa wanamaanishwa waumini wote katika Kristo, ikijumuisha wanaume na wanawake.AT: "waumini wengi"

kiongozi wa wokovu wao

Mwanadishi anaongea wokovu kana kwamba ni sehemu ambayo Yesu anawaongoza waumini kuelekea katika sehemu hiyo. Hii inamaanisha Yesu ni mtu ambaye alitenda kwanza ili awaokoe wengine. AT:"yeye anayewaokoa watu"

mkamilifu/ timiza

kukua kiroho na kufundishwa kikamilifu kunaongelewa kana kwamba mtu alikuwa akifanywa mtimilifu, pengine mtimilifu katika viungo vya mwili wake.

Hebrews 2:11

Maelezo ya Jumla:

Nukuu hii ya kinabii inatoka katika Zaburi ya Mfalme Daudi.

yeye anaye dhabihu

yeye anayewafanya wenzake watakatifu" au " "yeye awafanyae wengine kujtenga na dhambi"

walio takaswa

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji: AT: "wote anao wafanya watakatifu" au" wale anaowasafisha kutoka katika dhambi.

kuwa na chanzo kimoja

ambaye ni chanzo hicho ni nani inaweza kusemwa kwa ufasaha. AT: "muwe na chanzo, Mungu mwenyewe" au" muwe na yule yule.

haoni aibu

"Yesu haoni aibu"

haoni aibu kuwaita ndugu

maneno mawili hasi yanamaanisha atawafanya kama ndugu zake. AT: "anafurahishwa kuwaita ndugu"

Nitalitangaza jina langu kwa ndugu zangu

"Jina" hapa linamaanisha heshima ya mtu na kile walichokifanya. AT: "Nitatangaza kwa ndugu zangu mambo makuu uliyoyafanya"

kutoka katika asili/ kundi moja

"wakati waumini wanakuja pamoja kumwabudu Mungu"

Hebrews 2:13

Maelezo Jumla:

Nabii Isaya aliandika nukuu hizi

Na tena

"Na nabii aliandika andiko katika sura nyingine kuhusu kileKristo achokisema kuhusu Mungu:" (URD)

watoto... watoto wa Mungu

Hii inaongea wale wanaoamini katika Kristo kana kwamba ni walikuwa watoto wa Mungu.AT: wale walio kama watoto wangu...wale ambaao ni sawa na watoto kwa Mungu"

waliishi maisha yao yote katika utumwa.

Fungu hili la maneno limeelezwa na hurejea utumwa kwa hofu ya kifo

wanashiriki damu na mwili

maneno "mwili" na "damu" inamaanisha asili ya wanadamu." AT: "wote ni wanadamu"

"Yesu pia alishiriki mambo hayo hayo"

"Yesu alikuwa mwanadamu kama wao"

kwa kupitia kifo

kifo hapa kinaweza kuelezewa kama tendo. AT: "kwa kufa"

"alikuwa na nguvu ya kifo

kifo" hapa kinaweza kuelezewa kama tendo.AT: " alikuwa na kuvungu kuwafanya watu kufa"

Hii ilikuwa ili kwamba aweze kuwafanya huru wale wote ambao kupitia hofu ya kifo waliishi maisha ya utumwa

Hofu ya kifo inaongelewa kana kwamba ilikuwa utumwa. Kumuondolea mtu hofu inaongelewa kana kwamba ni kumfungua mtu kutoka utumwani.AT: "Hii ilikuwa ili kwamba awafungue watu wote. Kwa sababu tuliishi kama watumwa kwa sababu tulikuwa tukiogopa kufa"

Hebrews 2:16

mbegu ya Ibrahimu

Wana wa Ibrahimu wanaongelewa kana kwamba walikuwa mbegu yake. AT: "wana wa Ibrahimu"

ilikuwa ni muhimu kwake

"ilikuwa ni muhimu kwa Yesu"

kama ndugu zake

Neno "ndugu" hapa linamaanisha watu kwa ujumla. AT: "kama wanadamu"

ili alete msamaha wa dhambi kwa watu

Kifo cha Yesu msalabani kinamaanisha kwamba Mungu anaweza kusamehe dhambi. AT: "ili kwamba afanye uwezekano wa Mungu kusamehe dhambi za watu."

alijaribiwa

Hii inaweza kusema katika mfumo tendaji. AT: " Shetani akamjaribu"

wanaojaribiwa

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: "ambao shetani anawajaribu"

Hebrews 3

Waebrania 03 Maelezo kwa jumla

Muundo na mpangilio

Watafsiri wengine wamewaka kila msitari wa ushairi kulia kuliko maandishi mengine ili isomeke kwa urahisi. ULB inafanya hivi na ushairi katika 3:7-11,15, ambayo ni maneno kutoka Agano la Kale.

Dhana muhimu katika sura hii

Ndugu

Huenda mwandishi anatumia neno "ndugu" kuashiria Wakristo waliokua kama Wayahudi.

Mifano muhimu za usemi katika sura hii

Fanya mioyo yenu iwe ngumu

Mtu anayefanya moyo wake kuwa ngumu ni yule ambaye hatamsikiliza ama kumtii Mungu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

Maswali ya hadith

Mwandishi anatumia maswali ya hadithi kama njia ya kuwaonya wasomaji wake. Yeye pamoja na wasomaji wake wanajua majibu ya maswali haya na mwandishi anajua kwamba wakati wasomaji watafikiria juu ya majibu ya haya maswali, watatambua kwamba wanatakikana kumsikiliza Mungu na kumtii.

<< | >>

Hebrews 3:1

Sentensi Unganishi:

Hili ni onyo la pili na ni refu na liko katika undani na linajumuisha sura ya 3 na 4. Mwandishi anaanza kwa kwa kuonyesha kwamba Kristo ni bora zaidi ya Musa mtumishi wake.

ndugu watakatifu

Neno "ndugu" linamaanisha wakristo wenza, inajumuisha wanaume kwa wanawake. AT: "kaka na dada watakatifu" au "ndugu watakatifu wenzangu"

mnashirika katika mwito wa mbinguni

"Mbinguni" hapa ina mwakilisha Mungu. AT: "Mungu ametuita pamoja"

mtume

Neno hili linamaanisha mtu aliyetumwa. Katika kifungu hiki hakimaanishi mtume kati ya wale kumi na wawili. AT: "aliyetumwa"

ya ukiri wetu

hii inaweza kusemwa ili kwamba nomino dhaniwa "kutubu" inelezea kama kitenzi "tubu." AT: "ambaye tunayemtubia" au "ambaye katika yeye tunaamini"

katika nyumba ya Mungu

Waebrania ambao Mungu amejifunua kana kwamba ilikuwa ni nyumba halisi. AT: "kwa watu wote wa Mungu"

Yesu amefinywa

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: "Mungu amemfanya Yesu"

yeye ajengaye kila kitu

Matendo ya Mungu ya uumbaji wa ulimwengu yanaongelewa kana kwamba amejenga nyumba.

kila nyumba imejengwa na mtu

Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji. AT: "kila nyumba ina mtu aliyeijenga"

Hebrews 3:5

Hakika/ na

Hili neno linaanzishwa ulinganifu kati ya Musa na Kristo. Hili neno linaweza kuachwa katika tafsiri, kama sio muhimu.

Katika nyumba nzima ya Mungu

Waebrania ambao Mungu alijifunua mwenyewe wanaongelewa kana kwamba zilikuwa ni nyumba halisi. Tazama vile ulivyo tafasiri kama ulivyofanya 3:1.

Alikuwa ni ushuhuda kuhusu vitu

Pengine neno hili linamaanisha kwa kazi zote za Musa. AT: "Maisha na kazi za Musa zilielekeza kwenye vitu"

Viliongelewa katika wakati ujao

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: " Yesu angesema katika siku zijazo"

Mwana

Hiki ni cheo muhimu kwa Yesu, Mwana wa Mungu.

mtumishi katika nyumba ya Mungu

Hii inaongea kuhusu watu wa Mungu kana kwamba zilikuwa nyumba halisi. AT: "ambaye anatawala juu ya watu wa Mungu"

Sisi ni nyumba yake

Hii inaongea kwa watu wa Mungu kana kwamba ni nyumba halisi. AT: "Sisi ni watu wa Mungu"

kama tukiendelea kushikilia "ujasiri" wetu na tumaini letu lenye fahari

"ujasiri" na "tumaini lenye fahari" ni dhaaniwa na inaweza kusemwa kama vitenzi. AT: "tutaendelea katika ujasiri na furaha na kutumaini Mungu kufanya kile alichoahidi"

Hebrews 3:7

Sentensi Unganishi:

Onyo hapa ni ukumbusho kwamba kutokuamini kwa Waisraeli kuliwafanya wote kutoingia katika nchi ambayo Mungu alikuwa amewahidi. Kutokuamini kwao kulionyeshwa vizuri katika Kutoka 17:1, walipo mlalamikia Musa na kuwa na mashaka juu ya Mungu kama alikuwa pamoja nao.

Maelezo ya Jumla:

Nukuu hii inatoka katika Agano la Kale katika Zaburi.

kama mkisikia sauti yake

Amri za Mungu kwa Waisraeli zinaongelewa kana kwamba aliwakuwa amewapa katika sauti ya kusikika. AT: "kama mtasikia Mungu akiongea"

Msifanye mioyo yenu kuwa migumu

Ugumu wa moyo unaongelewa kana kwamba ni moyo halisi umefanywa kuwa mgumu. AT: "msiwewenye mioyo migumu"

kama katika uasi wakati wa kujaribiwa jangwani

Hapa "uasi" na "kujaribiwa" yanaweza kuelezewa kama vitenzi. AT: "kama vile na mababu zenu walivyo muasi Mungu na kumjaribu jangwani"

Hebrews 3:9

Maelezo ya Jumla:

Nukuu hii inatoka katika Zaburi.

Mababa

"zenu" hapa linamaanisha watu wa Israeli

kwa kunijaribu

Mungu ndiye anayeongea

miaka arobaini

"miaka 40"

Sikufurahishwa

"Nilikuwa na hasira" au "sikufurahia kabisa"

mara zote wanapotoshwa katika mioyo yao

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: "mara zote wanaenda katika njia zisizomfurahisha Mungu"

mioyoni mwao

Neno "mioyo" inamaanisha akili au tamaa za

Wamevijua njia zangu

Hii inaongelewa katika hali ya kuyafanya maisha ya mtu kana kwamba ni zilikuwa ni njia. AT: "Hawaelewi jinsi nilivyowataka waishi katika maisha yao"

Hawataingia katika pumziko langu

Amani na ulinzi uliotolewa na Mungu unaongelewa kana kwamba zilikuwa pumziko ambalo angeweza kuwapa, na kama zilikuwa ni sehemu ambayo watu wangeweza kwenda. AT: "Hawataingia kamwe katika sehemu ya pumziko" au "sitawaruhusu kupata baraka zangu za pumziko"

Hebrews 3:12

ndugu

Hili linatulejesha kwa ndugu Wakristo, ikijumuisha jinsia zote mbili za kiume na kike. AT: "kaka na dada" au "waumini wenza"

Hakutakuwa na mtu yeyote aliye na moyo mwovu usioamini

moyo unaongelewa hapa kana kwamba ni akili ya mtu, sehemu ya utashi ya mtu. AT: "mtu yeyote kati yenu asiache kuamini katika Mungu"

Moyo ambao unageuka kinyume na Mungu

Moyo mtu unaongelewa kana kwamba nimtu mzima, ambaye angeweza kuacha kufuata njia sahihi. AT: "na unaacha kumtii Mungu aishie"

Mungu aishie

"Mungu wa kweli ambaye kweli anaishi"

kama iitavyo "leo"

"wakati nafasi inapatikana"

Hakuna mmoja miongoni mwenu moyo wake utfanywa mgumu kwa udanganyifu wa dhambi.

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: "udanganyifu wa dhambi haufanyi moyo mgumu wa mtu yeyote kati yenu"

hakunammoja kati yenu moyo wake utafanywa kuwa mgumu kwa udanganyifu wa dhambi

kutokuwa msikivu kunatazamwa kana kwamba kuwa mgumu au kuwa na moyo mgumu. Ugumu wa moyo ni matokeo ya udanganyifu wa dhambi. Hii inaweza kutiwa neno ili kwamba nomino dhaniwa "udanganyifu" inaelezewa kama kitenzi "danganya." AT: "hakuna mtu miongoni mwenu atanganywa na dhambi na kutokuwa msikivu" au "usitende dhambi, ukijidanganya mwenyewe na kutokuwa msikivu"

Hebrews 3:14

Maelezo ya Jumla:

Hii inaendelea kutoka Zaburi ile ile ambayo pia ilinukuliwa katika 3:7.

Kwa sababu tumekuwa

"Tumekuwa" hapa inamaanisha wote, mwandishi na wasomaji,

kama tutaendelea kushikilia ujasiri wetu katika yeye

"kama tukiendelea kutumaini katika yeye kwa ujasiri"

kutoka mwanzo

"tangu mwanzo tulipoanza kuamini katika yeye"

hadi mwisho

Hii ni namna ya kusema kwa upole ikimaanisha mtu anapo kufa.AT: "hadi tunakufa"

imesemwa

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: "mwandishi aliandika"

Leo, ukisikia

Amri ya Mungu kwa Waisraeli zinaongelewa kana kwamba aliwapa katika hali ya kusikia. AT: "kama utasikia Mungu anaongea." Tazama kama ulivyo tafsiri 3:7.

kama katika kuasi

"Uasi" hapa unaweza kusemwa kama kitenzi. AT: "kama vile mababa zako walivyo muasi Mungu." Tanzama ulivyo tafsiri 3:7.

Hebrews 3:16

Maelezo ya Jumla:

Neno "wao" linamaanisha kwa kutotii kwa Waisraeli, na "sisi" inamaanisha mwandishi na wasomaji.

Ni wakina nani walio msikia Mungu na kuasi? Si wale waliokuja kutoka Misri kupitia Musa?

Mwandishi anatumia maswali kudundisha wasomaji wake. Maswali haya mawili yanaweza kuunganishwa kama sentensi moja, kama itahitajika. AT: "wale wote waliokuja na Musa kutoka Misri walimsikia Mungu, lakini bado waliasi."

Ni akina nani ambao Mungu aliawakasirikia kwa miaka arobaini? Sio wale waliotenda dhambi, ni miili ya kina nani iliyanguka jangwani/ nyikani?

Mwandishi anatumia maswali kuwafundisha wasomaji wake. Maswali haya mawli yanaweza kuunganishwa na kuwa swali moja, kama litahitajika. AT: "Mungu alikuwa na hasira kwa miaka 40 na wale waliotenda dhambi na kuwaacha wafe nyikani."

hawakuweza kuingia katika raha yake

Amani na ulinzi ambao Mungu vinaomgelewa kana kwamba ni pumziko alilowapa, na kama kwama vilikuwa ni sehemu za kwenda. AT: "hawataingia sehemu ya pumziko" au "hawatapata baraka zake za pumziko"

kwa sababu ya kutokuamini kwao

"kutokuamini" inaweza kusemwa kama kitenzi "tumaini." AT: "kwa sababu hawakuweza kumtumaini"

Hebrews 4

Waebrania 04 Maelezo kwa jumla.

Muundo na mpangilio

Sura hii inaelezea kwa nini Yesu ni Kuhani Mkuu kuliko wote

Watafsiri wengine wametenga kila msitari wa ushairi kulia kuliko maandishi mengine ili isomeke kwa urahisi. ULB inafanya hivi na ushairi katika 4:3-4,7, ambayo ni maneno kutoka Agano la Kale.

Dhana muhimu katika sura hii

Mapumziko ya Mungu

Neno "mapumziko" linaonekana kuashiria vitu viwili katika sura hii. Inaashiria mahali ama wakati Mungu atawaruhusu watu wake kupumzika kutokana na kazi zao (Waebrania 4:3), ama inaashiria kupumzika kwa Mungu siku ya Saba (Waebrania 4:4).

<< | >>

Hebrews 4:1

Sentensi Unganishi

Sura ya 4inaendeleza onyo lililoanza katika sura ya 3:7.Mungu kwa kupitia mwandishi anawapa waumini pumziko ambalo pumziko la Mungu katika uumbaji dunia ni picha.

kati yenu asiwepo hata mmoja atakayeweza kuonekana kushindwa kuifikia ahadi ya kuingia katika pumziko la Mungu iliyobaki kwa ajili yenu

Ahadi ya Mungu inaongelewa kana kwamba ilikuwa ni zawadi iliyoachwa baada ya Mungu kuwatembelea watu. AT: "mmoja wenu asishindwe kuingia katika pumziko la Mungu , ambalo alituahidi".

kuingia katika pumziko la Mungu

Amani na ulinzi uliotolewa na Mungu huongelewa kana kwamba vilikuwa ni pumziko ambalo anaweza kuwapa, na kana kwamba vilikuwa ni sehemu ambayo watu wangeweza kwenda. AT: "kuingia katika sehemu ya pumziko" au "kupata baraka za pumziko la Mungu.

Kwani tumekuwa na habari njema kama walivyokuwa nazo

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: "Kwa kuwa tulisikia habari njema kama walivyosikia"

kama walivyo

walivyo hapa linamaanisha mababu/mababa wa Kiebrania ambao walikuwa hai wakati wa Musa.

Lakini ujumbe ule haukuwafaa wale ambao hawakuungana katika imani pamoja na wale walio tii

"Lakini ujumbe ule haukuwafaa wale ambao hawakuungana na watu walio amini na kutii." Mwandishi anaongea kuhusu makundi mawili ya watu, wale waliopokea agano la Mungu kwa imani, na wale walio sikia lakini hawakuamini.

Hebrews 4:3

Maelezo ya Jumla:

Nukuu ya kwanza hapa (Kama nilivyoapa...) inatoka katika Zaburi, na nukuu ya pili (Mungu akapumzika...) inatoka katika Maandiko ya Musa, na ya tatu (Hawataingia...) inatoka katika Zaburi.

Sisi tulioamini

"sisi tulioamini"

watakao ingia katika pumziko hilo

Amani na ulinzi alioutoa Mungu vinaongelewa kana kwamba vilikuwa ni pumziko ambazo anaweza kuwapa, na kana kwamba ilikuwa ni sehemu ambayo watu wangeenda.

Kama alivyo sema

"Kama vile Mungu alivyosema"

Kama nilivyo apa katika hasira yangu

"Kama nilivyo apa wakati nilipokuwa nimekasirika sana"

Hawataingia kwenye pumziko langu

Amani na ulinzi uliotolewa na Mungu vinaongelwa kana kwamba zilikuwa pumziko la kuwapa, na kana kwamba vilikuwa ni sehemu ambayo watu wangeweza kwenda.

kazi yake ya uumbaji ilimalizika

Hii inaweza kuwekwa katika mfumo tendaji. AT: "alimaliza uumbaji" au "alimaliza kazi zake za uumbaji"

tangu mwanzo wa dunia/ ulimwengu

Mwandishi anaongelea dunia kana kwamba ni jengo lililowekwa kwenye kwenye msingi.

siku ya saba

Hii inasimama kama badala ya "saba"

Hebrews 4:6

bado imewekwa kwa baadhi kuingia katika pumziko

Amani na ulinzi uliotolewa na Mungu vinaongelwa kana kwamba zilikuwa pumziko la kuwapa, na kana kwamba vilikuwa ni sehemu ambayo watu wangeweza kwenda. Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji.AT: "Mungu bado anaruhusu baadhi ya watu kuingia katika sehemu yake ya pumziko.

kama mtasikia sauti yake

Amri za Mungu kwa Waisraeli zinaongelewa kana kwamba alikuwa amewapa kwa sauti. AT: "kama mtasikia Mungu akiongea"

msifanye mioyo yenu kuwa migumu

kutosikia kunaongelewa kana kwamba ni moyo ulikuwa umwefanya kuwa mgumu. AT: "Msiwe wenye mioyo migumu." Tafsiri kama ulivyofanya 3:7.

Hebrews 4:8

Sentensi Unganishi:

Mwanadishi anawaonya waumini wasiache kumtii Mungu, bali waiingie katika pumziko ambalo Mungu anawapa. Anawakumbusha kwamba neno la Mungu litawashuhudia na kwamba wanaweza katika maombi kwa ujasiri na kwamba Mungu atawasaidia

kama Yoshua angekuwa amewapa pumziko

Amani na ulinzi uliotolewa na Mungu vinaongelwa kana kwamba zilikuwa pumziko la kuwapa, na kana kwamba vilikuwa ni sehemu ambayo watu wangeweza kwenda. AT: "kama Yoshua angewaleta Wasraeli kwenye sehemu ambayo Mungu angewapa pumziko"

tuwe na shauku

Amani na ulinzi uliotolewa na Mungu vinaongelwa kana kwamba zilikuwa pumziko la kuwapa, na kana kwamba vilikuwa ni sehemu ya kuingia. AT: "tunapaswa kufanya kila kitu ili tuingie katika mpumziko mahali alipo"

wataanguka katika aina ya kutotii ambao walifanya

kutokutii kunaongelewa kana kwamba ni mtu mzima ambaye angeweza kuanguka katika ajali.

Hebrews 4:12

neno la Mungu li hai

"Neno la Mungu" hapa linamaanisha kila kitu ambacho Mungu ameongea kwa wanadamu iwe kwa kuongea au kwa kupitia ujumbe ulioandikwa.

lina hai na lina nguvu

Hii inaongelea neno la Mungu kana kwamba linaishi. Inamaanisha wakati Mungu anapoongea ni kuna nguvu na utendaji kazi.

lina ukali kuliko upanga wowote wenye makali mawili

upanga wenye makali. upanga wenye makali kuwili ni rahisi kukata kupitia mwili wa mtu. Neno la Mungu lina nguvu katika kuonyesha kilichomo katika moyo na mawazo ya watu.

Na huchoma hata kufikia kugawanya nafsi na roho, na viungo kutika uboho.

Hii inaendelea kuongea kuhusu neno la Mungu kana kwamba ulikuwa ni upanga. Upanga hapa ni mkali sana kiasi kwamba unaweza kukata na kugawa viungo vya mwanadamu ambavyo ni vigumu pengine visivyo wezekana kugawanyika.

nafsi na roho

Haya ni maneno mawili tofauti lakini sehemu za mwanadamu ambazo hazina mwili. "Nafsi" ndiyo inamfanya mtu kuwa hai na "roho" ni sehemu ya mtu ambayo inamsababisha kuweza kumjua na kumwamini Mungu.

viungo kutoka maboho

"kiungo" ndicho kinacho shikilia mifupa miwili pamoja. "uboho" ni sehemu ya kati ya mfupa.

kuweza kufahamu

Hii inaongea neno la Mungu kana kwamba ni mtu ambaye angewezakujua kitu.

mawazo na makusudi ya moyo

Hii inaongea kuhusu moyo kana kwamba ni sehemu ya kati ya mawaazo na hisia za mwanadamu.

Hakuna kilichoumbwa kilichojificha katika uso wa Mungu

Hili linaweza kuelezwa katika mfumo tendaji. AT: "hakuna kitu kilichoumbwa na Mungu kinaweza kujificha mbele zake"

kila kitu kiko wazi

Hii inaongelea kila kitu kana kwamba ni mtu amesimama wazi au boksi lililo wazi.

wazi na iliyo wazi

Kimsingi maneno haya mawilii yanamaanisha kitu kimoja na kusisitiza kwamba hakuna kitu chochote kilichojificha mbele za Mungu.

kwa macho ya yule tutakaye toa hesabu

Mungu anaongelwa kana mwamba ana macho ya nyama. AT" Mungu atatuhukumu kulingana na vile tulivyoishi"

Hebrews 4:14

aliyeziingia mbingu

"aliyeingia mahali alipo Mungu"

Mwana wa Mungu

Hiki ni cheo muhimu kwa Yesu.

tushikilie sana imani zetu

imani na tumaini vinaongelewa kana kwamba ni vitu ambavyo mtu angeweza kuvikumbatia.

hatuna kuhani mkuu ambaye hawezi kutuhurumia... Badala, tunaye

Maneno haya yakukanusha yanalenga kuonyesha kwamba Yesu ni mwenye huruma kwa watu . AT: " tunaye kuhani mkuu anayeweza kutuhurumia...Kweli tunaye"

kiti cha enzi cha neema

"kiti cha enzi cha Mungu, pale palipo na neema" au "pale Mungu, ambaye ni neema, ameketi katika kiti chake cha enzi"

yeye ambaye kwa njia zote amekuwa akijaribiwa kama sisi

Hii inaweza kusemwa katikamfumo tendaji. AT: "yeye ambaye amevumilia majaribu katika kila hali tunayoipitia" au "ambaye movu amekuwa akimjaribu katika kila njia anavyotujaribu"

hana dhambi

"hakutenda dhambi"

kiti cha enzi cha neema

"kwemye kiti cha enzi cha Mungu palipo na neema." "kiti cha enzi" hapa kina maanisha utawala wa Mungu kama mfalme.

ili kwamba tupokee rehema na kupata neema ya kutusaidia wakati wa hitaji.

"rehema" na "neema" hapa vinaongelewa kana kwamba ni vitu ambavyo vinaweza kupewa au kupatikana.

Hebrews 5

Waebrania 05 Maelezo kwa jumla

Muundo na mpangilio

Sura hii inaendeleza mafundisho ya sura iliyopita.

Watafsiri wengine wametenga kila msitari wa ushairi kulia kuliko maandishi mengine ili isomeke kwa urahisi. ULB inafanya hivi na ushairi katika 5:5-6.

Dhana muhimu katika sura hii

Kuhani mkuu

Ni kuhani mkuu tu angetoa dhabihu ili Mungu asamehe dhambi na kwa hivyo lazima Yesu alikuwa kuhani Mkuu. Sheria ya Musa iliamuru kwamba kuhani mkuu atoke kwa kabila la Walawi lakini Yesu alitoka kabila la Yuda.Mungu alimfanya kuhani kama Melikizedeki aliyeishi nyakati za Abarahamu kabla ya kuwepo kabila la Walawi.

Mifano muhimu za usemi katika hi sura

Maziwa na chakula kigumu

Mwandishi anazungumzia Wakristo ambao wako tu na uwezo wa kuelewa vitu rahisi kumhusu Yesu kana kwamba walikuwa watoto wachanga wanaokunywa tu maziwa na hawawezi kulaa chakula kigumu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

<< | >>

Hebrews 5:1

Sentensi Unganishi:

Mwandishi anafafanua dhambi za makuhani wa Agano la Kale, na kisha anaonyesha kuwa Kristo anao ukuhani bora, na hautokani na ukuhani wa haruni, bali unaotokana na ule waMelkizedeki.

chaguliwa kutoka miongoni mwa watu

Hii inaweza kusemwa katika muundo tendaji. AT: "ambaye Mungu anachagua kutoka miongoni mwa watu"

amechaguliwa

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: "Mungu huachangua/ huteuwa"

kusimama badala ya/ kutenda kwa niaba ya watu

"kuwawakilisha watu"

wajinga na waovu

"wale walio wajinga waovu"

waovu

watu ambao wanaishi katika njia za dhambi"

amezungukwa na udhaifu.

udhaifu wa kuhani mkuu unaongelewa kana kwamba ni nguvu zilizo mzunguka

udhaifu

hapa inamaanisha hamu ya kutenda dhambi.

pia anahitajika

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. "Mungu pia anamhitaji"

Hebrews 5:4

Sentensi Unganishi:

Nukuu hii inatoka katika Zaburi katika Agano la Kale

achukuaye heshima hii

Heshima inaongelewa kana kwamba ni kitu ambacho Mungu kukichukua katika mkono wake.

achukue heshima hii

heshima au sifa na heshima ambazo watu walimpa kuhani mkuu husimama kwa ajili ya majukumu yake

aitwe/ ameitwa na Mungu, kama alivyokuwa Haruni

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: "Mungu alimwita kama alivyomwita Haruni"

Mungu alisema kwake

"Mungu alisema kwake"

" Wewe ni mwanangu, leo nimekuwa Baba yako."

kimsingi neno hili linamaanisha kitu kimoja. Tazama ulivyotafsiri 1:4.

Hebrews 5:6

Maelezo ya Jumla:

Unabi huu unatoka katika Zabur ya Daudi.

kama asemavyo/ pia anasema

kwa yule ambaye Mungu anaongea naye inaweza kusemwa wazi. AT: "pia anamwambia Kristo"

katika sehemu nyingine

"katika sehemu nyingine katika maandiko"

mfano wa Melkizedeki

Hii inamaana kuwa Kristo kama kuhani ana vitu vinavyofananana Melkizedeki kama kuhani.

Hebrews 5:7

kipindi chake katika mwili

Neno siku/ kipindi zinasimama badala ya kipindi cha muda. Na "mwili" unasimama badala ya maisha ya Yesu duniani, AT: "wakati aliposhi duniani"

maombi na kuombea/

Kimsingi maneno haya yanamaanisha kitu kimoja

kumwokoa kutoka kwenye kifo

Kifo kinaongelewa kana kwamba ilikuwa ni sehemu kKristo angezuiliwa kutoingia, au kana kwamba ni sehemu ambayo angeokolewa.

alisikiwa

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: "Mungu alimsikia"

mwana

Hiki ni cheo muhimu kwa Yesu, Mwana wa Mungu.

mambo yaliyomtesa

mateso kana kwamba ni vitu.

Hebrews 5:9

Sentensi Unganishi:

Katika mst wa11 mwandishi anaanza onyo lake la tatu. Anawaonya hawa wauminikuwa bado ni wachanga wa kiroho na kuwatia moyo kujjifunza neno la Mungu ili kwamba waweze kutambua jema na baya.

alifanywa mkamilifu

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: "Mungu alifanya mkamilifu"

alifanya mkamilifu

hapa inamaanisha kuweza kufanywa mtu mzima kiroho, kuwa tayari kumtii Mungu katika nyanja zote za maisha.

Alikamilishwa na kwa njia hii alifanyika kwa kila mtu amwaminiye kuwa sababu ya wokovu wa milele

Nomino dhaaniwa "wokovu" inaweza kusemwa kama kitenzi. AT: "hivyo anawaokoa wale wote wanaomtii na kuwafanya waishi milele"

kwa kutengwa na Mungu

Hii inaweza kusems katika mfumo tendaji. AT: "Mungu alimtenga" au "Mungu alimteua"

baada ya zamu ya Melkizedeki

hii inamaanisha kwamba Kristo kama kuhani ana vitu vinavyofanana na Melkizedeki kama kuhani.

Tuna mengi ya kusema

Ingawa mwandishi anatumia neno la wingi lakini inaweza kuwa anamaanisha yeye mwenyewe.

ninyi ni wavivu wa kusikia

uwezo wa kuelewa na kutii kunaongelewa kana kwamba ulikuwa ni uwezo wa kusikia. Na uwezo wa kusikia kunaongelewa kana kwamba ilikuwa ni chuma cha kilichohabika katika matumizi.

Hebrews 5:12

kanuni za msingi

kanuni hapa zinamaanisha maelekezo au viwango vya kufanya maamuzi. AT:"msingi wa ukweli"

Mnahitaji maziwa

mafundisho kuhusu Mungu ambayo ni rahisi kuelewa yanaongelewa ni maziwa, chakula pekee ambacho watoto wachanga wanaweza kula. AT: "mmekuwa watoto na mnaweza kunywa maziwa pekee"

si chakula kigumu

mafundisho ambayo ni magumu kuelwa yanaongelewa kana kwamba kilikuwa ni chakula kigumu, kifaacho kwa watu wazima.

anywaye maziwa

anywaye linasimama ka kunywa.

kwa sababu bado ni mtoto

hii inaongelea waumni ambao wanaweza kuelewa mafundisho rahisi ya injili kana kwamba walikuwa watoto halisi.

ambao kwa sababu ya uzoefu wao katika kutofautisha haki na ubaya wamefundishwa kutambua jema na ovu.

watu walifundishwa kuelwa jambo wanaelezewa kana kwamba ni uwezo wa kuelewa umefundishwa.

Hebrews 6

Waebrania 06 Maelezo kwa jumla

Dhana muhimu kwa sura hii

Agano la Kiabrahamu

Katika agano Mungu alifanya na Abrahamu, Mungu aliahidi kuwafanya uzao wake kuwa taifa kubwa. Aliahidi pia kuwakinga uzao wa Abrahamu na kuwapa ardhi yao. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#covenant)

<< | >>

Hebrews 6:1

Sentensi Unganishi:

mwandishi anendele na kile Waebrania waumini walipaswa kufanya ili wawe wakristo wakomavu. Anawakumbusha mafundisho ya msingi.

tukiacha tulichojifunza kwanza kuhusu ujumbe wa Kristo, twapaswa kuwa na juhudi kuelekea kwenye ukomavu

Hii inaongelea kuhusu mafundisho ya msingi kana kwamba yalikuwa ni mwanzo wa safari na mafundisho makomavu kana kwamba ni mwisho wa safari.

tusiweke tena misingi ya toba kutoka katika kazi zisizo na uhai na imani katika Mungu,

Mafundisho ya msingi yanaongelewa kana kwamba yalikuwa ni jengo ambalo mjenzi alianza kwa kuweka msingi. AT: "tusirudie mafundisho ya awali... ya imani katika Mungu"

kazi zisizo na uhai

matendo ya dhambi yanaongelwa kana kwamba yalitoka katika ulimwengu wa wafu.

ala misingi ya mafundisho ya...hukumu ya milele

Mafundisho ya msingi yanaongelea kana kwamba yalikuwa ni jengo ambalo mjenzi wake alianza kwa kuweka msingi. AT: "wala mafundisho ya msingi... uzima wa milele"

kuwekea mikono

Huduma hii iliwekwa kwa kumtenga mtu kwa huduma au nafasi maalum.

Hebrews 6:4

wale ambao waliipata nuru

uelewa unaongelewa kana kwamba ilikuwa ni kupatiwa nuru. AT: "wale ambao awali walielewa ujumbe kuhusu Kristo"

ambao walionja kipawa cha mbinguni

kuonja wokovu kunaongelewa kana kwamba ni kuoonja chakula. AT: walionja nguvu ya Mungu ya kuokoa"

kufanywa kuwa washirika wa Roho Mtakatifu,

Roho Mtakatifu ambaye anakuja kwa waumini, anaongelewa kana kwamba ni chombo ambacho watu wangeweza kushiriki. AT: "waliopoke Roho Mtakatifu"

ambao walionja uzuri wa neno la Mungu

Kujifunza neno la Mungu kunaongelewa kana kwamba ilikuwa ni kuonja chakula. AT: "waliojifunza neno zuri la Mungu"

nguvu za wakati ujao

Hii inamaanisha nguvuza Mungu wakati ufalme wake utakapo kuwa umetimilka duniani kote. kwa mantiki hii "nguvu" ina maanishaMungu mwenyewe, ambaye anamiliki nguvu zote.

kisha wakaanguka

kupoteza uaminifu kwa Mungu kunaongelewa kana kwamba anguko la kimwili.AT: "walioacha kuamini katika Mungu"

haiwezekani kuwarejesha tena katika toba

"Haiwezekani kuwarejesha tena kwenye toba"

wamemsulubisha Mwana wa Mungu kwa nafsi zao

watu wanapoondoka kwa Mungu ni kana kwamba wanamsulubisha tena Yesu.

Mwana wa Mungu

Hiki ni cheo muhimu ambacho kinaelezea uhusiano kwa Mungu.

Hebrews 6:7

ardhi iliyopokea mvua inyeshayo mara kwa mara juu yake

ardhi inufaikayo na mvua nyingi inaongelewa kana kwamba ni mtu aliyekunywa maji mengi ya mvua.

ikatoa mazao muhimu

Ardhi izaayo mazao inaongelewa kana kwamba iliwazalia.

kwa hao waliofanya kazi katika ardhi

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: "kwa wale kwa ajili yao mtu aliandaa ardhi"

ardhi hupokea baraka kutoka kwa Mungu

Mvua naa mazao vinaonekana kama ushahidi kama Mungu amemsaidia mkulima. Ardhi inaongelewa kana kwamba ni mtu ambaye angeweza kupokea baraka za Mungu.

ipo katika hatari ya kulaaniwa

Hii inaongelea "laana" kana kwamba ni ilikuwa ni sehemu ambayo mtu angeweza kukaribia. AT: "iko katika hatari ya Mungu kuilaani.

Mwisho wake ni kuteketezwa

Mungu atasababisha kila kitu katika shamba hilo kuteketea.

Hebrews 6:9

tunashawishiwa

ingawa mwandishi anatumia nomino ya wingi "Tuna" mara nyingi anamaanisha yeye mwenyewe.

ambo mazuri yawahusuyo

Hii inamaana kuwa wanafanya vizuri kuliko wale walio mkataa Mungu, wasiomtii yeye, na hawawezi tena kutubu ili kwamba awasamene.

mambo yahusuyo wokovu

Nomino dhaaniwa "wokovu" inaweza kuwekwa kama kitenzi.

Kwa kuwa Mungu si dhalimu hata asahau

Maneno haya yanamaanisha kuwa Mungu katika haki yake atakumbuka mambo mazuri ambayo watu wake wameyafanya.

jina lake

"Jina" lake lina maanisha Mungu

Hebrews 6:11

tunatamani sana

Ingawa mwandishi anatumia wingi lakini anamaanisha yeye mwenyewe.

bidii

uangalifu, kazi ngumu

mpaka mwisho

AT: "mpaka mwisho wa maisha yako"

kwa ajili ya uhakika wa ujasiri

"ili kuwa na uhakika timilifu kuwa mtapokea kile ambacho Mungu amewaahidi ninyi"

waigaji

"muigaji" ni mtu ambaye ana nakili tabia ya mtu mwingine.

kuzirithi ahadi

kupokea kile ambacho Mungu alichowaahidi waumini kinaongelewa kana kwamba ilikuwa wanarithi kitu na utajiri kutoka kwa mwanafamilia. AT: " pokea kileambacho Mungu amewaahidi"

Hebrews 6:13

Alisema

Mungu akasema

Nitakuongeza zaidi

Neno "ongeza" hapa linasimama kwa uzao. AT: "Nitakupa uzao mwingi'

Kile kilichoahidiwa

Hii inaweza kusemwa katika muundo tendaji. AT: " Kile ambacho Mungu alimuahidi"

Hebrews 6:16

kwa warithi wa ahadi

kwa watu ambao Mungu amewawekea ahadi wanaongelewa kana kwamba walikuwa warithi kitu na utajiri kutoka kwa mwanafamilia. AT: "kwa wote ambao wangepokea kile alichoahidi"

kwa kusudi zuri lisilobadilika

"kwamba kusudi lake halitabadilika kamwe" au "kwamba mara zote atafanya kile alichosema atafanya"

kwa vitu viwili visivyobadilika

Hii ina maana ahadi ya Mungu na kiapo cha Mungu. Wala hivi haviwezi kubadilika.

ambavyo katika hivyo haiwezekani kabisa Mungu kudanganya

Vikanushi hivi viwili vinaweza kumaanisha kwamba Mungu atasema kweli kuhusu hali hii. AT:"ambayo mara zote Mungu husema kweli"

sisi, tuliokimbilia

Waumini, ambao wanatumaini katika Mungu kwa yeye kuwalinda, wanaongelewa kana kwamba walikuwa wanakimbilia kwenye sehemu salama. AT: ""sisi, ambao tuliomtumaini yeye"

lile lililowekwa mbele zetu

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: "kile ambacho Mungu ameweka mbele zetu"

Hebrews 6:19

Sentensi Unganishi:

Baada ya kumaliza onyo lake la tatu na maneno ya kuwatia moyo waumini, mwandishi wa Waebrania anaendeleza ulinganifu wake wa Yesu kama kuhani dhidi ya kuhani Melikizedeki.

kama nanga salama na tegemewa ya roho zetu

Kama vile nanga inanyoshikilia mtumwi kutoenda sehemu nyingine ndani ya maji, Yesu anatuweka sisi sehemu salama katika uwepo wa Mungu.

ujasiri uingiao sehemu ya ndani nyuma ya pazia

Ujasiri unaongelewa kana kwamba ni mtu ambaye angeweza kwenda katika mahali patakatifu pa patakatifu pa hekalu.

sehemu ya ndani

Hii ilikuwa ni sehemu ya ndani ya hekalu.Ilidhaniwa kuwa ndiyo sehemu Mungu alikuwa akikaa miongoni mwa watu wake. Katika sura hii sehemu hii inasimama kama mbingu na chumba cha kiti cha enzi cha Mungu.

kama mtangulizi wetu

Ukweli kwamba Yesu alikufa na kufufuka, na kwamba sasa yuko na Mungu Baba, inaonyesha kwamba sisi tunaoamini katika yeye tutapata mambo yaleyale.Yesu anaoglewa hapa kana kwamba ni mtu ambaye anakimbia mbele yetu na kwamba tunamfuata.

kwa mfano wa Melikezedeki

Hii ina maana kuwa Kristo kama kuhani ana vigezi sawa na vya kuhani Melikizedeki,

Hebrews 7

Waebrania 07 maelezo kwa jumla

Muundo na Mpangilio

Watafsiri wengine wametenga kila msitari wa ushairi kulia kuliko maandishi mengine ili isomeke kwa urahisi. ULB inafanya hivi na ushairi katika 7:17,21, ambayo ni maneno kutoka Agano la Kale.

Dhana muhimu katika sura hii

Kuhani mkuu

Ni kuhani mkuu tu angetoa dhabihu ili Mungu asamehe dhambi na kwa hivyo lazima Yesu alikuwa kuhani Mkuu. Sheria ya Musa iliamuru kwamba kuhani mkuu atoke kwa kabila la Walawi lakini Yesu alitoka kabila la Yuda.Mungu alimfanya kuhani kama Melikizedeki aliyeishi dhabihui za Abarahamu kabla ya kuwepo kabila la Walawi.

<< | >>

Hebrews 7:1

Sentensi Unganishi

Mwandishi wa kitabu cha Waebrania anaendeleza ulinganifu wake juu ya Yesu kama kuhani na kuhani Melikizedeki.

Salem

Hili ni jina la mji.

Abrahamu anarudi kutoka kuwauwa wafalme

Hii ina maanisha wakati Abrahamu na watu wake walipoenda na kuyashinda majeshi ya wafalme wanneili kumwokoa benamu yake, Lutu, na familia yake.

ilikuwa kwake

"Ilikuwa kwa Melikizedeki"

mfalme wa haki... mfalme wa amani

"mfalme wa haki... mfalme wa amani"

Hana baba, hana mama, hana wazazi, wala mwanzo wa siku wala mwisho wa maisha yake

Inawezekana kufikiri kutoka katika ukurasa huu kwamba Melikizedeki hakuzaliwa wala hakufa. Ingawa, ni kama inamaanisha mwandishi anamaanisha kwamba Maandiko hayaarifu chochote kuhusu wazazi wa Melkizedeki, kuzaliwa, au kifo.

Hebrews 7:4

Sentensi Unganishi:

Mwandishi anasema kwamba ukuhani wa Melikizedeki ni bora kuliko wa ukuhani wa haruni na anakumbusha kuwa ukuhani wa Haruni haukukamilisha chochote.

huyu mtu alikuwa

'Melikizedeki alikuwa"

kwa upande mmoja...lakini kwa upande mwingine

maneno haya yametumika kulinganishwa vitu viwili. Lugha yako inaweza kuwa na namna ya msisitizo kwamba mwandishi anaweka ulinganifu. Au unaweza kutumia "kwa upande mwingine"

Wana wa Lawi ambao hupokea ukuhani

Mwandishi anasema hili kwa sababu sio wana wote wa Lawi walikuwa makuhani.

kutoka kwa watu

"kutoka kwa watu wa Israeli"

kutoka kwa ndugu zao

Neno ndugu hapa linamaanisha kuwa wote wanahusiana kupitia kwa Abrahamu.

wao, pia wanatoka katika mwili wa Abrahamu

Hii ni namna nyigine ya kusema walikuwa wana wa Abrahamu.

ambao uzao wake haukutoka kwao

"ambao hawakuwa wana wa Lawi"

yeye aliyekuwa na ahadi

Mambo ambayo Mungu aliahidi kufanya kwa ajili ya Abrahamu yanaongelewa kana kwamba vilikuwa ni vitu ambavyo angeweza kumiliki.

Hebrews 7:7

mtu mdogo hubarikiwa na mkubwa

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji: AT: "Mtu wa muhimu humbariki mtu asiye wa muhimu kama yeye"

katika jambo hili... katika jambo lile

Maneno haya hutumika katika kulinganisha ukuhani wa Lawi na ukuhani wa Melikizedeki. Lugha yako unaweza kuwa kunaweza kuwa na namna ya kusisitiza kwamba mwandishi anafanya ulinganifu.

imeshuhudiwa kwamba anaendelea kuishi

haijaandikwa katika maandiko kwamba kwamba Melikizedeki anakufa. Mwandishi wa kitabu cha Waebrania anaandika kukosekana kwa taarifa ya kifo cha Melikizedeki kana kwamba bado anaendelea kuishi. Hii inaweza kuelezewa katika muundo tendaji. AT: "andiko linaonyesha kuwa anaendele kuishi:

Lawi... alikuwa katika mwili wa baba yake

kwa kuwa Lawi alikuwa hajazaliwa bado, mwandishi kana kwamba bado alikuwa katika mwili wa Abrahamu. Kwa jinsi hii mwandishi anatia hoja kuwa Lawi alilipa zaka kwa Melikizedeki kupitia Abrahamu.

Hebrews 7:11

sasa

Hii haimanishi "kwa wakati huu," imetumika kuvuta usikivu kwa kipengele muhimu kinachofuata.

kungekuwa na hitaji gani jingine zaidi la kuhani mwingine kuja kwa mfano wa Melikizedeki, na wala sio kwa mfano wa Haruni?

Swali hili linasisitiza kwamba haikutegemewa kwamba kuhani angeweza kuja kwa mfano wa Melikizedeki.

kuinuka

"kuja" au "kutokeza"

kwa mfano wa Melikizedeki

Hii ina maana kuwa Kristo kama kuhani ana sifa zifananazo na kuhani Melikizedeki.

na sio kutoka kwa namna ya Haruni

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: "na sio kuwa kwa jinsi ya Haruni" au "ambaye ni kuhani sio kwa mfano wa Haruni"

Kwa kuwa pindi ukuhani unapobdilishwa, sheria nayo ni lazima ibadilishwe.

Hii inaweza kutamkwa katika mfumo tendaji. AT: " kwa kuwa Mungu alipobdilishwa ukuhani, pia alipaswa kubadlisha sheria"

Hebrews 7:13

Kwa ambaye

Hii ina maanisha Yesu.

ambaye mambo mambo haya yanasemwa kuhusu yeye

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: "ambaye ninaongea kuhusu yeye

Sasa

Hii haimanishi "wakati huu," lakini linatumika kuvuta usikivu kwa ajili ya kipengele muhimu kinachofuata.

Bwana wetu alizaliwa katika Yuda

Haya maneno "Bwana wetu" linamaanisha Yesu.

kutoka Yuda

"kutoka katika kabila la Yuda"

Hebrews 7:15

Maelezo ya Jumla:

Nukuu hii inatoka katika Zaburi ya mfalme Daudi

haya tuyasemayo ni wazi hasa

" tunaweza kuelewa hata zaidi." "tuna" inamaanisha mwandishi na watu anaowaandikia.

ikiwa kuhani mwingine atatokea

"kama kuhani mwingine atakuja"

kwa mfano wa Melikizedeki

Hii ina maana kwamba kristo ana sifa sawa na kuhani Melikizedeki.

kwa msingi wa sheria zinazohusiana na uzao wa mwili

wazo la huzao wa mtu linaongelewa kana kwamba ilikuwa inashughulika na mwili wa mtu.

lakini katika msingi wa nguvu ya maisha yasiyo haribika

Neno " alifanyika kuhani" linaeleweka. AT: "lakini alikuwa kuhani kwa msingi wa nguvu ya maisha ambayo hayatakoma"

Kwa sababu maandiko yanashuhudia kuhu yeye

Hii inaongelewa kana kwamba andiko ni mtu ambaye angeweza kushuhudia kuhusu kitu.

kwa mfano wa Melikizedeki

Hii ina maanisha kwamba Kristo kama kuhani ana sifa sawa na za kuhani Melikizedeki.

Hebrews 7:18

kulikuwa na amri ya kwanza kutanguliwa

Mungu aliifanya amri yake ya kwanza kutofaa"

sheria haikukamilisha chochote

sheria inaongelewa kana kwamba alikuwa ni mtu ambaye angeweza mutenda.

kuna utangulizi wa ujasiri mzuri

"Mungu ametupa hoja bora ya kuwa na ujasiri"

kuna utangulizi wa ujasiri bora iliyombele yetu ambayo kwa hiyo tunamkaribia Mungu

Ujasiri kwa wakati ujao unaongelewa kana kwamba ni kitu ambacho kutia hicho mtu lazima amkaribie Mungu.

tunamkaribia Mungu

Kumwabudu Mungu na kuwa na upendeleo wake vinaongelewa kana kwamba ni tendo la kumkaribia yeye.

Hebrews 7:20

maelezo ya Jumla:

Nukuu hii inatoka katika Zaburiya Daudi kama mstari wa 17

hii haikutokea pasipo kula kiapo

Tendo la kula kiapo linaongelewa bila kusema ni nani aliyekula hicho kiapo. Japo kuwa alikuwa Mungu.

kwa kiapo kilichotolewa kwa ambaye alimwambia

hii inawea kusemwa katika mfumo tendaji. AT:"kwa sababu Mungu aliapa kwake kwa kusema"

Hebrews 7:22

Sentensi Unganishi:

Mwandishi anawahakikishia aumini hawa wa Kiyahudi kwamba Kristo na ukuhani ulio bora kwa sababu anaishi milele na makuhani wote waliotoka kwa Haruni walikufa.

dhamana

"uhakika" au "ukweli"

kwa hakika au kwa upande mwingine

maneno haya yametumika kulinganisha mambo mawili. Lungha yako inaweza kuwa na msisitizo kwamba mwandishi anafanya ulinganifu.

kifo huuhuzuia kutodumu

Hii inaweza kusemwa katika muundo tendaji. AT: '"mwishowe wanakufa na hawawezi kuendelea"

ana ukuhani udumuo/ haubadiliki

kazi ya kikuhani inaongelewa kana kwamba ni chombo ambach Yesu alikimiliki. AT: "yeye ni kuhani asiye badilika"

Hebrews 7:25

Kwa hiyo

unaweza kufafanunua "neno "Kwa hiyo" linachomaanisha. AT: " Kwa sababu Kristo ni kuhani wetu mkuu anayeishi milele"

wale wanaomkaribia Mungu

"wale wanaokuja kwa Mungu kwa sababu ya kile Yesu alichofanya"

ametukuka zaidi kuliko mbingu

"na Mungu amemuinua juu kupita mbingu." Mwandishi anaongelea kumiliki heshima zaidi na nguvu zaidi ya mtu yeyote kana kwamba ni nafasi ambayo ni zidi ya vitu vyote. AT: "na Mungu amempaheshima na nguvu kuliko mtu yeyote"

Hebrews 7:27

Maelezo ya Jumla:

Maneno "Yeye" na "mwenyewe" yanaamaniisha Kristo. Neno "yake" linamaanisha makuhani wakuu wa duniani.

sheria uteua

Neno sheria hapa ni neno linalosimama kwa niaba ya Mungu, ambaye alianzisha sheria. Waisraeli waliteuwa makuhani wao kwa mjibu wa sheria.

wamaume waliokuwa dhaifu

wanaume waliokuwa dhaifu kiroho" au "wanaume ambao ni wadhaifu kw dhambi"

neno la kiapo, ambalo lilikuja baada ya sheria, lilimweka Mwana

"baada ya kuwapa sheria, Mungu aliapa kwa kiapo na kumteua Mwanawe"

kwa neno la kiapo

neno "kiapo" limepewa nafsi na linaelezewa kana kwamba ni mtu ambaye aliongea.

Mwana

Hiki ni cheo muhimu kwa Yesu, Mwana wa Mungu.

aliyefanywa kuwa mkamilifu

"aliyekamilishwa kumtii Mungu na kuwa mkomavu"

Hebrews 8

Waebrania 08 Maelezo kwa jumla

Muundo na mpangilio

Mwandishi anamalizia kwa kufafanua jinsi gani na ni kwa nini Yesu ndiye kuhani mkuu muhumu. Halafu anaanza kuzungumzia jinsi agano jipya ni bora kuliko agano Mungu alifanya na Musa. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#covenant)

Watafsiri wengine wametenga kila msitari wa ushairi kulia kuliko maandishi mengine ili isomeke kwa urahisi. ULB inafanya hivi na ushairi katika 8:8-12, ambayo ni maneno kutoka Agano la Kale.

Dhana muhimu katika sura hii.

Agano jipya

Mwandishi anaelezea jinsi Yesu ameanzisha agano jipya ambalo ni bora kuliko agano Mungu alianzisha na wana wa Israeli. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#covenant)

<< | >>

Hebrews 8:1

Sentensi Unganishi:

Baadaa ya mwandishi kuonyesha ukuhani wa Kristo ulivyo bora kuliko ukuhani wa duniani, anaonyesha kuwa ukuhani wa duniani ulikuwa ni mfano wa mambo ya mbinguni. Kristo ana huduma iliyo bora, au agano lililobora.

Sasa

Hii haimaanishi ni "wakati huu," lakini neno hili limetumika kuvuta usikivu kwa kipengele muhimu kinachofuata.

tunasema

Ingawa mwandishi anatumia wingi "tuna" kimsingi anaongea yeye mwenyewe.AT: "Ninasema" au "ninaandika"

aliketi kwa mkono wa kuume

Neno "mkono wa kuume" linamaanisha sehemu ya heshima. AT: "aliketi katika sehemu ya heshima"

katika kiti cha enzi mbinguni

Neno "Ukuu" linamaanisha Mungu, na kiti chan enzi linamaanisha utawala wa Mungu kama mtawala,

hema ya kweli ambayo Bwana, sio mwanadamu, aliliweka

watu walijenga hema za dunianikwa kutumia ngozi za wanyama zilizofungwa katika nguzo za mbao, na zikawekwa kwa namna ya hema. Hema ya kweli hapa inamaanisha hema ya mbinguni ambayo Mungu ameitengeneza.

Hebrews 8:3

Kwa kuwa kila kuhani mkuu huteuliwa

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji.AT: "kwa kuwa Mungu huteua kila kuhani'

Sasa

hII haimaanishi "wakati huu," lakini imetumika ili kuvuta usikivu kwenye kipengele muhimu kinachofuata.

kwa mjibu wa sheria

"kama Mungu anavyotaka katika sheria"

nakala na kivuli

Haya maneno yana kimsingi yana maana moja ili kusisitiza kwamba hema ilikuwa ni sura halisi ya hema ya mbinguni.

kivuli cha mambo ya mbinguni

Mwandishi anaongea hekalu la duniani, ambalo ni nakala ya hekalu la mbinguni, kana kwamba ilikuwa ni kivuli.

Kama vile Musa alivyo onywana Mungu wakati alipokuwa

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. "kama vile Mungu alivyomwonya Musa wakati Musa alipokuwa"

alipotaka kuanza kujenga hema

Musa hakujenga hema yeye mwenyewe. Aliwaamuru watu kuijenga. AT: "alitaka kuwaawamuru watu kuijenga hema"

"Tazama," Mungu akasema, "kwamba wewe...mlima

unaweza kutoa nukuu. AT: "Mungu akasema, 'tazama kwamba wewe... mlima""

tazama

"Hakikisha"

muundo

"kwa muundo"

ilioonyeshwa

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: "Ile niliyokuonyesha"

juu ya mlima

Mlima inanaanisha mlima Sinai.

Hebrews 8:6

Sentensi Unganishi:

Sehemu hii inaanza kwa kuonyesha kwamba agano jipya ni bora kuliko agano la kale la Israeli na Yuda.

Kristo amepokea

"Mungu amempa Kristo"

huduma iliyo bora zaidi. kama alivyo mpatanishi wa agano bora

"huduma iliyo bora zaidi, kama Kristo alivyo mpatanishi wa agano bora"

mpatanishi wa agano bora

Hii ina maanisha kuwa Kristo alisababisha agano bora kuendelea kati ya Mungu na wanadamu.

ambalo liko katika ahadi bora

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: ''ni agano hili ambalo Mungu alilifanya kulingana na ahadi zilizo bora" au "Mungu aliahidi vitu bora wakati alipofanya agano hili"

Aagano la kwanza... agano la pili

Haya maneno "kwanza" na "pili" ni namba za kawaida. AT:" agano la zamani ... agano jipya"

halingekuwa na makosa

"ingekuwa kamilifu"

Hebrews 8:8

Maelezo ya Jumla:

Ktika nukuu hii nabii Yeremia alikuwa amesema agano jipya ambalo Mungu angefanya

na watu

"na watu wa Israeli"

Angalia

"Tazama" au "Sikiliza" au "Kuwa na tahadhari kwa lile ninalotaka kuwaambia."

Siku zinakuja

Ziku zijazo zinaongelewa kana kwamba zinatembea kumkabiri mzungumzaji. AT:"ktakuwa na wakati"

nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda

Watu wa Israeli na watu wa Yuda wanaongelewa kana kwamba wao ni nyumba. AT:"watu wa Isareli na watu wa Yuda"

Niliwachukua kwa mkono na kuwaongoza kutoka katika ardhi ya Misri.

Picha inawakilisha upendo mkuu wa Mungu na kujali kwake.

hawakuendelea katika katika agano langu

Kutii agano la Mungu kunaongelewa kana kwamba mtu alipaswa kuendelea katika hilo. AT: "hawakutii agano langu"

Hebrews 8:10

Maelezo ya Jumla:

Nukuu hii inatoka kwa nabii Yeremia.

nyumba ya Israeli

Watu wa Israeli wanaongelewa kana kwamba walikuwa ni nyumba.

baada ya siku hizo

"baada ya wakati huo"

nitaweka sheria zangu mioyoni mwao

Sheria za Mungu zinaongelewa kana kwamba ni vyombo ambavyo vingeweza kuwekwa mahali fulani. Uwezo wa watu kufikiri kunaongelewa kana kwamba ni sehemu.AT: "Nitawawezesha kuelewa sheria zangu"

Pia nitaziandika mioyoni mwao

Mioyo ya watu ilifikiriwa kuwa kituo cha uaminifu kwa Mungu, na imeongelewa kana kwamba ni ukurasa ambao ungeweza kuandikwa.

nitakuwa Mungu wao

"Nitakuwa Mungu wanae mwabudu"

watakuwa watu wangu

"watakuwa watu ambao ninawajali"

Hebrews 8:11

Maelezo ya Jumla:

Hii inaendeleza nukuu kutoka kwa nabii Yeremia.

Hawatafundishana kila mmoja na jirani yake, na kila mtu na ndugu yake, akisema, 'Mjue Bwana.'

Nukuu hii ya moja kwa moja inaweza kuengelewa kana kwamba ni nukuu isiyo ya moja kwa moja. AT: "Hawatahitaji kuwafundisha jirani zao au ndugu za kunijua"

jirani... ndugu

Haya maneno mawili yanalenga Waisraeli wenzao.

Kumjua Bwana...wote watanijua mimi

Neno "kujua" hapa linasimama kwa maana ya kutambua.

kwa matendo yao yasiyo ya haki

Hili linasimama kwa ajili ya watu waliofanya matendo haya yasiyo ya haki.

Sitazikumbuka dhambi zao tena

Neno "kumbuka" linamaanisha "sitafikiri kuhusu dhambi hizo"

Hebrews 8:13

liko karibu na kutowekaka

"limekaribia kabisa kutoweka" au "litatoweka hivi karibuni"

Hebrews 9

Waebrania 09: Maelezo kwa jumla

Muundo na Mpangilio

Sura hii inaonyesha jinsi Yesu ni bora kuliko hekalu na sheria na masharti yake. Sura hii itakuwa ngumu kuelewa iwapo vitabo vitanu vya kwanza vya Agano la Kale havijatafsiriwa.

Dhana muhimu katika sura hii

Agano la urithi

Agano la urithi ni hati ya kisheria ambayo huelezea kile ambacho kitafanyikia mali ya mtu baada ya kifo chake.

Damu

Katika Agano la kale, Mungu alikuwa ameamuru Waisraeli kutoa dhabihu ili dhambi zao zisamehewe. Kabla hawajatoa dhabihu hizi, walipaswa kuwaua wanyama na siyo kutoa tu miili ya wanyama hao lakini pia damu zao. Kutoa damu ni tamathali ya kumuua binadamu ama mnyama.Mungu alipeana uhai na damu yake kama dhabihu/kafara alipowaruhusu watu kumuua.Mwandishi wa Waebrania anasema kwamba hii dhabihu ni bora kuliko dhabihu ya agano la kale.(Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#covenant)

Kurudi kwa Kristo

Yesu atarudi kumaliza kazi aliyoianzisha wakati alipokufa ili Mungu angewasamehe watu dhambi zao. Atamalizia kuwaokoa watu wanaomngojea.(Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#save)

Maswala mengine ya utata katika tafsiri ya sura hii

Agano la Kwanza

Hii inaashiria agano ambalo Mungu alifanya na Musa. Hata hivyo, kabla hajafanya agano hili, Mungu alikuwa amefanya agano na Abrahamu. Lakini hili lilikuwa ni agano la kwanza ambalo Mungu alifanya na watu wa Israeli. Unaweza amua kutafsiri "agano la kwanza" kama "agano la awali."

<< | >>

Hebrews 9:1

Sentensi Unganishi:

Mwandishi anawaweka wazi hawa waumini wa Kiyahudi kwamba sheria na hema ya agano la kale vilikuwa ni picha ya agano bora na jipya.

Sasa

Hii inaonyesha sehemu mpya ya fundisho.

agano la kwanza

Tafsiri hii kama ulivyotafsiri sura ya 8:6

ilikuwa na taratibu

"ilikuwa na maelekezo ya ndani" au "ilikuwa na miongozo"

kwani

mwandishi anaendeleza mazungumzo kutoka sura ya 8:6

hema ilitengenezwa

Hema ilijengwa na kuwa tayari kwa matumizi

kinara cha taa, meza na mkate wa wonyesho

Vyombo hivi vyote vinafuatwa neno la linaloonyesha upekee wa vyombo. Kwa sababu mwandishi anadhani kwamba wasomaji wake tayari wanafahamu kuhusu vitu vyombo hivi.

mkate wa wonyesho

mkate wa wonyesho mbele za Mungu au mkate ambao makuhani waliuwakilisha kwa Mungu.

Hebrews 9:3

nyuma ya pazia la pili

pazia la kwanza kulikuwa na ukuta wa nje wa hema, hivyo pazia la pili lilikuwa ni pazia la pili kati ya mahali patakatifu na mahali patakatifu pa patakatifu.

pili

Hii ni nambaya kawaida ya namba mbili

ndani yake

"Ndani ya sanduku la agano"

Fimbo ya Haruni iliyoota maua

Hii ina maanisha wakati Mungu alipoonyesha kwa watu wa Israeli kwamba alikuwa amemchagua Haruni kama kuhani kwa kuichipusha maua fimbo ya Haruni.

kuchipua

"kuwa na maua" au "kuchipua" au "ilikuwa na kuendelea"

mbao za agano

"Mbao" ni vipande bapa vya mawe vilivyokuwa na maandishi juu yake. Hizi zinamaanisha mbao za mawe ambazo ziliandkwa amri kumi.

makerubi walifunika juu

wakati Waisraeli walipokuwa wakitengeneza sanduku la agano, Mungu aliwaamuru Waisraeli kuchonga makerubi wawili wanatazamana pamoja na mbao zao zigusa juu ya kifuniko upatanisho cha sanduku la agano. Hapa vinaongelewa kana kwamba kama vinaweka kivuri kwenye sanduku la agano.

ambao hatuwezi

Ingawa mwandishi anatumia kiwakilishi cha wingi "tuna" kimsingi anasema kwa nafsi yake mwenyewe.

Hebrews 9:6

Baada ya vitu hivi kuandaliwa

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji.AT: "Baada ya makuhani kuandaa vitu hivi"

na sio pasipo damu

Hii inaweza kusemwa katika muundo tendewa. AT: "na mara zote alileta damu"

damu

Hii ni damu ya dume na mbuzi ambazo kuhani mkuu alipaswa kudhabihu siku ya upatanisho.

Hebrews 9:8

njia ya kuingia mahali patakatifu zaidi ilikuwa haijafunuliwa bado

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: "Mungu alikuwa bado hajaifunua njia ya sehemu takatifu zaidi"

mahali patakatifu zaidi

Maana zinazowezekana: 1) chumba cha ndani cha hema duniani au 2) Uwepo wa Mungu mbinguni.

hema la kwanza bado lilikuwa limesimama

Maana zinazowezekana: 1) "chumba cha nje cha hema bado kinasimama" au 2) "hema ya duniani na taratibu za dhabihu zilikuwa zikiendelea."

kielelezo

"Hii ilikuwa ni "picha" au "Hii ilikuwa ni alama"

kwa muda uliopo

"kwa sasa"

ambayo kwa sasa yanatolewa

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. "ambayo sasa makuhani wanatoa"

haviwezi kukamilisha dhamiri ya anayeabudu/ mwabudu

Mwandishi anaongelea dhamiri ya mtu kana kwamba ni kilikuwa ni chombo ambacho kilikuwa kikifanywa bora zaidi. Dhamiri ya mtu ni ni ujuzi wa kujua baya na jema. Pia ni uelewa wake kama amekosa au amefanya jema. Na kama akifahamu kwamba ametenda baya tunasema anajisikia hatia.

taratibu kwa ajili ya mwili

Mwili hapa unamaanisha mwili wa binadamu." AT: "taratibu za mwili"

taratibu za kimwili

"desturi za maisha ya kimwili"

Hizi zilikuwa desturi za kimwili ambazo zilizotolewa

"Mungu aliandaa taratibu zote hizi kwa ajili ya mwili"

ambazo zilizotolewa hadi mpangilio mpya ungeweza kuumbwa

Hii inawezakusemwa katika mfumo tendaji. AT: "Kwamba Mungu alitoa hadi alipoumba mpangilio mpya"

Mpangilio mpya

"agano jipya"

Hebrews 9:11

Sentensi Unganishi:

Baada ya kufafanua huduma ya hema la agano chini ya sheria ya Mungu, mwandishi anaweka bayana kwamba huduma ya Kristo chini ya agano jipya ni bora pia kwa sababu imefunikwa kwa damu yake. Ni bora pia kwa sababu Kristo ameingia hekalu la kweli, ambalo ni uwepo wa Mungu mbinguni, badala ya ya kuingia, kama makuhani wakuu, ndani ya hema ya duniani, ambayo kimsingi ilikuwa ni nakala isiyo timilifu.

Vitu vizuri

Hii haimaanishi vitu vinavyoshikika. Inamaanishavitu vizuri ambavyo Mungu ameahidi katika agano lake jipya.

hema kuu na ukamilifu zaidi

Hii inamaanisha hema la mbingunini muhimu zaidi na timilifu zaidi ya hema ya duniani.

ambayo haikufanywa kwa mikono ya binadamu

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: "ambayo haikufanywa kwa mikono ya binadamu"

mikono ya binadamu

"Mikono" inamanisha mtu.

mahali patakatifu zaidi

Uwepo wa Mungumbinguni unaongelewa kana kwamba kana kwamba ilikuwa sehemu takatifu zaidi, chumbacha ndani cha hekalu.

Hebrews 9:13

kunyunyiziwa kwa majivu kwa hao ambao hawajatakaswa

Kuhani angemimina kiasi kidogo cha majivu kwa watu wasiosafi.

je si sana zaidi damu ya Yesu...kuosha nafsi zetu kutoka katika matendo mafu ili kumtumikia Mungu aliye hai?

Mwandishi anatumia nukuu kusisitiza kwamba dhabihu ya Kristo ilikuwa na nguvu. AT: Hivyo hakika damu ya Kristo itatusafisha nafsi zetu hata zaidi kutoka katika kazi/ matendo mafu na kumtumikia Mungu aliye hai! Kwa sababu, kupitia kwa kupitia Roho wa milele, alijitoa mwenyewe pasipo hatia kwa Mungu.

damu ya Kristo

"damu" ya Yesu inasimama kwa kifo chake.

kusafisha dhamiri zetu

"Dhamiri" hapa inamaanisha mtu kujisikia hatia. Kwa sababu Yesu alijidhabihu yeye mwenyewe, waumini hawapaswi tena kujisikia hatia kwa ajili ya dhambi zao walizozifanya kwa sababu amewasamehe.

waa

Hii ni dhambi ndogo au kosa la kimaadili hapa linaongelewa kana kwamba lilikuwa dogo,doa lisilo la kawaida kuharibu juu ya mwili wa Kristo.

safisha

"kusafisha" linasimama kwa tendo la nafsi zetu kupokea msamaha wa kutokuwa na hatia kwa ajili ya dhambi tulizozitenda

hao walioitwa na Mungu

wale ambao Mungu amewateua au kuchaguliwa na kuwa watoto wake

Kazi/ matendo mafu

matendo mafu yanaongelewa kana kwamba yalikuwa yakitoka katika ulimwengu wa wafu.

Kwa sababu hii

"kama matokeo" au "kwa sababu hii"

Ni mjumbe/ mpatanishi wa agano jipya

Hii inamaanisha Kristo alisababisha agano jipya kati ya Mungu na wanadamu kuwepo.

agano la kwanza

tafsiri hii kama ulivyotafsiri 8:6

wale walioitwa

Hii inaweza kuelezwa katika mfumo tendaji. AT: "wale ambao Mungu aliowachagua kuwa wana wake"

urithi

upokeaji wa kile ambacho Mungu alikuwa amewaahidi waumini kunaongelewa kana kwamba ilikuwa ni kurithi kitu na mali kutoka katika mwanafamilia.

Hebrews 9:16

wosia

hati ya kisheria ambayo inamtaja mtu ambaye angepokea zile mali wakati mwenye mali akifa.

kifo cha mtu aliyetenda ni lazima kihakikishwe

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: "mtu ni lazima ahakikishe kwamba mtu aliweka wosia amekufa"

Hebrews 9:18

hivyo hata agano la kwanza halikuanzishwa pasipo damu

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: "Hivyo Mungu alianzisha hata lile agano la kwanza kwa damu"

agano la kwanza

Tafsiri hii kama ulivyotafsiri 8:6

damu

kifo cha wanyama waliotolewa dhabihu kunaongelewa kana kwamba hakukuwa na kitu kingine isipokuwa damu.

alichukua damu... pamojas na maji...na kunyunyiza...gombo... na watu wote

Kuhani alichovyawa hissopo katika damu na maji na kisha alikitikisa kijiti cha hissopo na kudondosha damu na maji juu ya magombo na watu.Kunyunyiza damu lilikuwa ni tendo la ishara lililofanywa na makuhani ambalo kwa hilo walipata faida ya agano kwa watu na vyombo. Na hapa upokelewaji wa gombo na watu vinafanywa upya.

hisoppo

mmea uliotumika katika ibada ya kunyunyiza

damu ya agano

"Damu" hapa linamaanisha kifo cha wanyama waliotolewa dhabihu ili kuftimiza matakwa ya agano.

Hebrews 9:21

alinyunyuzia

"Musa alinyunyuzia"

nyunyuzia

Kunyunyuzia kulikuwa ni tendo la ishara ambalo lilifanywa na makuhani ambalo kwa hilo walipata faida ya agano kwa watu na kwa viyombo.

Vyombo vyote vilivyotumiwa katika huduma

huu ni mkebe au chombo ambacho unaweza kubeba vyombo. Hii inamaanisha vyombo au kitu. AT: " vyombo vyote vilivyotumika katika huduma"

vilitumika katika huduma

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: "Makuhani walivitumia katika kazi zao"

karibia kila kitu kinatakaswa kwa damu

kufanya kitu kipokelewe na Mungu kunafanywa kana kwamba kitu hicho kilikuwa kinatakaswa. Wazo hili linaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: "Makuhani hutumia damu kusafisha karibia ila kitu"

damu

Hapa damu ya mnyama inaongelewa kuhusu kifo cha mnyama.

Hakuna msamaha wa dhambi pasipo kuwagika damu

Hapa "kumwaga damu" kunamaanisha kwa kitu kufa kama dhabihu kwa Mungu. mambo haya hasi yanaweza kumaanisha msamaha wote unapatikana kwa njia ya kumwaga damu.

msamaha

"msamaha wa dahmbi ya watu"

Hebrews 9:23

Sentensi Unganishi:

Mwandishi anasisitiza kwamba Kristo (sasa yuko mbinguni anatuombea) alipaswa kufa mara moja tu kwa ajili ya dhambi na kwamba atarudi duniani mara ya pili.

nakala ya vitu vya mbinguni vinapaswa kusafishwa kwa dhabihu ya hawa wanyama

"Makuhani wanapaswa kutumia dhabihu hii ya wanyama kusafisha nakala za vitu vya mbinguni"

vitu vya mbinguni vyenyewe vilipaswa visafishwe kwa dhabihu zilizo bora zaidi

Ile ni bora zaidi ya dahabihu zilizotumika kusafisha nakala za duniani. Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: "kama kwa vitu vya mbinguni vyenyewe, Mungu alipaswa kuvisafisha kwa dhabihu iliyo bora"

ilitengenezwa kwa mikono

"Mikono" hapa inamaanisha mwanadamu. AT: "ambayo wanadamu walitengeneza na"

ya kitu halisi

"sehemu ya kweli na takatifu ya patakatifu pa patakatifu"

Hebrews 9:25

Hakuingia kule

" Hakuingia mbinguni"

mwaka baada ya mwaka

"kila mwaka" au "mwaka baada ya mwa

na damu ya mwingine

Hii inamaanisha na damu ya mnyama wa kafara, na sio kwa damu yake mwenyewe.

na kama hiyo ilikuwa kweli/ sababu

"Kama alipaswa kutoa mara nyingi"

tangu mwanzo wa ulimwengu

Uumbaji wa dunia unaongelewa kana kwamba ni jengo na msingi wake ulikuwa sehemu ya kwanza kujengwa. AT: "tangu Mungu alipoanza kuiumba dunia"

amefunuliwa

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: "Mung amemfunua"

kuindoa dhambi kwa dhabihu yake mwenyewe

Hii inaongea kuhusu dhambi kana kwamba kilikuwa ni chombo ambach mtu angeweza kukiondoa. AT: "kumsababisha Mungu kusamehe dhambi kwa kujidhabihu mwenyewe"

Hebrews 9:27

Pia Kristo, ambaye alitolewa

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: "Pia Kristo, ambaye "aliyejitoa mwenyewe"

kuziondoa dhambi

Tendo la kutufanya wasio na hatia badala ya kuwa na hatia kwa ajili ya dhambi zetu kunaongelewa kana kwamba dhambi zetu zilikuwa vyombo ambavyo vinashikika ambavyo Kristo aliweza kuzibeba.

dhambi

dhambi inamaanishahatia ambayo watu waliyonayo mbele za Mungukwa sababu ya dhambi walizotenda.

Hebrews 10

Waebrania 10 Maelezo kwa jumla.

Muundo na mpangilio

Katika hii sura, mwandishi anamalizia kwa kufafanua jinsi sadaka ya Yesu ni bora kuliko sadaka zilizotolewa hekaluni.(Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lawofmoses)

Watafsiri wengine wametenga kila msitari wa ushairi kulia kuliko maandishi mengine ili isomeke kwa urahisi. ULB inafanya hivi na ushairi katika 10:5-7,:15-17, 37-38, ambayo ni maneno kutoka Agano la Kale.

Dhana muhimu katika sura hii

Hukumu ya Mungu na tuzo

Kuishi kitakatifu ni muhimu kwa Wakristo. Mungu atawajibisha watu jinsi walivyoishi maisha yao ya Kikristo. Ingawa hakutakuwa na hukumu ya milele kwa Wakristo, matendo yasiyo pendeza Mungu yatakuwa na matokeo. Zaidi ya hayo maisha ya uaminifu yatatuzwa. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#holy, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#godly and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faithful and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#reward)

Maswala mengine ya utata katika tafsiri ya sura hii.

Maana damu ya fahali na mbuzi haiwezi kamwe kuondoa dhambi" (Waebrania 10:4)

Dhabihu zenyewe hazikuwa na nguvu za kuokoa. Zilifanikiwa kwa sababu zilikuwa dhihirisho la imani ambayo ilitokana na aliyekuwa anatoa hiyo Dhabihu. ilikuwa ni sadaka ya Yesu inayofanya sadaka hizi "kuondoa dhambi". Kulingana na hayo, Mungu hataki sadaka iltolewao bila imani. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#redeem and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith)

"Agano nitakalofanya"

Haiko wazi iwapo huu unabii ulikuwa unatimizwa wakati mwandishi huyu alikuwa anaandika ama iwapo ungetimizwa baadaye. Mtafsiri aepuke kusema wakati muda wa agano hili inaanza. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#prophet and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#covenant)

<< | >>

Hebrews 10:1

Sentensi Unganishi:

Mwandishi anaonyesha udhaifu wa sheria na dhabihu zake, kwa nini Mungu aliwapa sheria, na utimilifu wa ukuhani mpya na dhabihu ya Kristo.

sheria ni kivuli cha mambo mema yajayo

Hii inaongewa kuhusu sheria kana kwamba kilikuwa ni kivuli. Mwandishi anaongea kwamba sheria haikuwa vitu vizuri ambavyo Mungu alikuwa ameviahidi. Ni sehemu ndogo tu ya mambo mazuri ambayo Mungu alipaswa kuyafanya.

si yale yaliyo halisi ya yale mambo yenyewe

" sio vitu halisi vyenyewe"

mwaka hadi mwaka

"kila mwaka"

dhabihu hizo zisingeweza kukoma kutolewa

Mwandishi antaumia swali kuelezea kwamba dhabihu zilikuwa na nguvu ya ukomo. "wangekuwa wameacha kudhabihu dhabihu"

ilikoma

"sitisha"

Kwa sababu hiyo

"kwa hali hiyo"

wakiwa wamesafishwa

Dhambi za watu zinaongelewa kana kwamba ziklikuwa zikioshwa ana kwa ana. AT: " Kama Mungu alikuwa tayari amekwisha samehewa dhambi zao"

wasingekuwa na utambuzi

"wangeweza kufahamu kuwa hawana hatia ya dhambi tena."

haiwezekani kwa damu mafahari na mbuzi kuziondoa dhambi

Dhambi zinaongelewa kana kwamba zikuwa vyombo ambavyo damu ya wanyama ingeweza kuziondoa. AT: "Kwa sababu haiwezekani kabisa Mungu kusamehe dhambi kwa kwa sababu ya damu ya mafahar na mbuzi.

damu ya mafahari na mbuzi

"Damu" hapa inamaanisha kwa wanyama hawa waliokuwa wanakufa kwa kama dhabihu kwa Mungu.

Hebrews 10:5

Maelezo ya Jumla:

Maneno ya Kristo alipokuwa duniani yalikuwa yamesemwa katika nukuu hii kutoka Zaburi ya Daudi.

ambayo ulitamani

"Wewe" hapa ni nafsi ya umoja na inamaanisha Mungu.

mliandaa

"kufanya tayari"

kisha nilisema

"Nilisema" inamaanisha Kristo

kama ilivyoandikwa katika gombo kuhusu mimi

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: " kama manabii walivyoandika katika gombo kuhusu mimi"

gombo

Hii inamaanisha maandiko au maandiko matakatifu.

Hebrews 10:8

Maelezo ya Jumla:

pamoja na kwamba anabadilisha maneno polepole, mwandishi anarudia nukuu hii kufoka Zaburi ya Daudi kusisitiza.

dhabihu...sadaka...au sadaka za kuteketezwa... dhabihu kwa ajili ya dhambi

Tafsiri maneno haya kama ulivyotafsiri 10:5

amabyo hutolewa

"ambayo makuhani hutoa"

Ona/tazama

"Tazama" au "sikiliza"

ameweka pembeni taratibu za awali

Jina la tendo dhaaniwa "taratibu"/ tendo hapa inamaanisha njia ya kudhabihu kwa ajili ya dhambi.Kusitisha kufanya kunaongelewa kana kwamba kilikuwa ni chombo ambacho kingeweza kuondolewa.

taratibu za awali... taratibu za pili

Maneno "kwanza" na "pili" ni namba za kawaida.AT: "taratibu za zamani ...taratibu mpya"

ili kuanzishe utaratibu wa pili

Kuanzisha njia ya pili ya kudhabihu inaongelewa kana kwamba kuanzisha utaratibu AT: "ill kutoa dhabihu kwa ajili ya dhambi kwa mara nyingine"

Tumetakaswa/ tumetengwa

"Mungu ametutakasa" au "Mungu ametuweka kwake kwa ajili yake"

tumekwisha kutengwa kwa Mungu kwa mapenzi yake

"Mungu alitaka Kristo kujitoa mwenyewe dhabihu na kwamba dhabihu ilishatutenga sisi kwa Mungu"

kupitia dhabihu ya mwili wa Yesu Kristo

"wakati Yesu Kristo alipotoa mwili wake kama dhambihu" au "kwa sababu Yesu Kristo aliudhabihu mwili wake"

Hebrews 10:11

kwa upande mwingine ... na kwa upande mwingine

Haya maneno yanatumika kulinganisha vitu viwili . Lugha yako inaweza kuwa na njia ya kusisitiza kwamba mwandishi anaweka ulinganifu. Au unaweza kutumia "Lakini."

siku kwa siku

"siku hadi siku" au "kila siku"

haiwezi kuziondoa dhambi

Hii inaongelea. dhambi kana kwamba ni chombo ambacho mtu anaweza kukiondoa. AT: "haiwezi kumfanya Mungu asamehe dhambi"

hadi maandui zake wamewkwa chini ya miguu yake

kuteswa kwa maadui wa Kristo kunaongelewa kana kwamba ni sehemu iliyotengenezwa kwa ajili yake kupumzishia migu yake. AT: "hadi Mungu atakapowaseta maadui wa Kristo na kuwa kana kiti cha miguu yake"

wale ambao wametengwa kwa Mungu

"wale ambao Mungu amewatenga kwa ajili yake mwenyewe"

Hebrews 10:15

Maelezo ya Jumla:

Hii ni nukuu kutoka kwa nabii Yeremia katika Agano la Kale.

pamoja nao

"amoja na watu wangu"

baada ya siku hizo

"wakati wa agano la kwanza na watu wangu ulipokwisha"

Nitaziweka sheria zangu ndani ya mioyo yao, na nitaziandika katika akili zao

Mioyo ya watu na akili vinaongelewa kana kwamba sheria ya Mungu ingeweza kuwekwa au kuandikwa juu yake. AT: "Nitawasababisha kuzielewa shria zangu na nitawasababisha kuzitii sheria zangu"

Hebrews 10:17

Maelezo ya Jumla:

Hii inaendeleza nukuu ya nabii Yeremia katika Agano la Kale

Sitazikumbuka dhambi zao na makosa yao

Hii ni sehemu ya pili ya ushuhuda wa Roho Mtakatifu (tazama 10:15). Kisha asema, "Sitazikumbuka dhambi zao na makosa yao."

Sitazikumbuka dhambi zao

"Sitazikumbuka dhambi zao"au "sitafikiri tena kuhusu dhambi zao"

Sasa

Hii haimaanishi "wakati huu," lakini imetumika kuvuta usikivu kwa kipengele kinachofuata.

mahali palipo na msamaha kwa mambo haya

"wakati Mungu aliposamehe mambo haya"

hakuna tena dhabihu yeyote kwa ajili ya dhambi

"watu wao hawahitajiki kutoa dhabihu kwa ajili ya dhambi"

Hebrews 10:19

Sentensi Unganishi:

Baada ya kuweka wazi kwamba kuna dhabihu moja kwa ajili ya dhambi, mwandishi anaendelea na picha ya patakatifu pa patakatifu katika hekalu, mahali ambapo kuhani mkuu aliweza kuingia kila mwaka na damu ya dhabihu

Ndugu

Hii inamaanisha kwa waumini wote katika Kristo awe mwanaume au mwanamke. "dada" au "waumini"

mahali patakatifu zaidi

Hii inamaanisha uwepo wa Mungu, sio mahali patakatifu zaidi katika hema ya zamani.

kwa damu ya Yesu

"Damu ya Yesu" inamanisha kwa kifo cha Yesu.

njia iliyo hai

pengine inamaana 1) Njia hii mpya kwa Mungu kwamba Yesu ametoa matokeo ndani ya waumini kuishi milele au 2) Yesu yu hai, na na ni njia ambayo waumini wanaingia kuingia katika uwepo wa Mungu.

kwa jinsi ya mwili wake

neno mwili hapa inasimama kama kwa mwili wa Yesu, na mwili wake unasimama kwa kifo chake the kujidhabihu. AT: "kwa jinsi ya mwili wake"

Tunaye kuhani Mkuu juu ya nyumba ya Mungu

Hii ni lazima itafsiriwe katika namna kuweka wazi kwamba Yesu ni "kuhani Mkuu."

juu ya nyumba

"Msimamizi wa nyumba"

nyumba ya Mungu

"watu wote wa Mungu"

Tumkaribie

Kumkaribia hapa inasimama kwa kumwabudu Mungu, kama kuhani alipaswa kwenda juu ya mimbali ili kudhabihu wanyama kwa Mungu.

mioyo imenyunyiziwa safi

"mioyo ambayo Mungu ameinyunyizia kwa damu ya Yesu na kuifanya safi"

mioyo yetu ikiwa imenyunyizwa na kutakaswa

"kana kwamba alifanya mioyo yetu safi kwa damu yake"

kunyunyiziwa

"kazi ya kuweka vitu kuwa safi"

baada ya mikono yetu kuwa imeoshwa kwa maji maji halisi

"kana kwamba alikuwa ameosha miili yetu kwa maji halisi"

miili yetu imeoshwa kwa maji halisi

Kama mtafasirianaelewa kwamba sentensi hii yanamaanishaubatizo wa Kikristo, hivyo maji ni maji halisi na sio mfano. Lakini kama maji yanachukuliwa kama maji, hivyo "halisi" inasimama kwa niaba ya usafi wa kiroho ambao ubatizo unaosemwa hapa umetimiliza. "Kuoshwa" kunasimama kama waumini kuwa kupokelewa na Mungu.

Hebrews 10:23

shikilia kwa udhabiti ungamo la tarajio la ujasiri wetu

"endelea kuwaambia watu kwamba tuna ujasiri kwa sababu tunaamini kuwa Mungu atatenda kile alichoahidi kutenda"

pasipo kugeukageuka/ kuyumba yumba.

pasipokuwa na kuwa na hakika" au "pasipokuwa na shaka"

Tusiache kukusanyika pamoja

"tusiache kujumuika pamoja kwa ajili ya ibada"

kadri mwonavyo siku inakaribia

"Kama mnavyofahamu kuwa Kristo atakuja hivi karibuni"

Hebrews 10:26

Sentensi Unganishi:

Mwandishi anatoa onyo la nne.

kwa makusudi

"kwa kukusudia"

baada ya kuwa tumepokea ujuzi wa kweli

Ujuzi wa kweli kunaongelewa kana kwamba ni chombo ambacho kinaweza kumpa mtu mmoja hadi mwingine. AT: "baaba ya kuwa tumejifunza kweli"

dhabihu ya dhambi haipo tena

"hakuna awezaye kutoa dhabihu ambayo Mungu atatusamehe dhambi zetu"

kweli

Ukweli kuhusu Mungu.

hakuna tena dhabihu kwa ajili ya dhambi

Hakuna mtu yeyote awezaye kutoa dhabihu mpya kwa sababu dhabihu ya Kristo ndiyo pekee inayofanya kazi.

dhabihu kwa ajili ya dhambi

"dhabihu kwa ajili ya dhambi" inasimama kama njia tendaji ya kudhabihu wanyama ili kuondoa dhambi"

ya hukumu

ya hukumu ya Mungu. ambayo, Mungu atahukumu.

ukali wa moto ambao utawateketeza adui wa Mungu

Ukali wa Mungu unaongelwa kana ni moto ambao ungechoma maadui wake.

Hebrews 10:28

wawili au watatu

Imepewa maana ya kwambahii inamaanisha "angalau wawili au watatu"

kiwango gani zaidi cha adhabu unafikiri kinamstahili...neema?

Mwandishi anasisitiza ukuu wa adhabu kwa wale wote wanaomkataa Kristo.

amemdharau mwana wa Mungu

Kutokumjali Kristo na kumtukana kunaongelewa kana kwamba mtu anakanyaga.

ambaye ameihesabu damu ya agano kama sio takatifu

Hii inaonyesha jinsi mtu alivyokanyaga Mwana wa Mungu. Kwa kuihesbu damu ya agano kama sio takatifu"

Mwana wa Mungu

Hili ni jina muhimu la cheo cha Yesu

damu ya agano

"damu" hapa inasimama kama kifo cha Kristo, ambacho kwa hicho Mungu alianzisha agano jipya.

damu ambayo kwa hiyo alitakaswa

"damu ambayo Mungu alimtakasa kwa hiyo"

Roho wa neema

"Roho wa Mungu anayetoa neema"

Hebrews 10:30

Maelezo ya Jumla:

Neno "tuna" linamaanisha kwa mwandishi na waumini wote. Nukuu hizi mbili zinatoka kwenye sheria ambayo Musa alitoa katika Agano la Kale.

kisasi ni juu yangu

kisasi kinaongelewa kana kwambani chombo ambacho kinatoka kwa Mungu, ambaye alikuwa na haki ya kufanya na kama alivyotaka na kile alichomiliki. Mungu anayo haki kulipa kisasi juuya maadui zake.

nitalipa

Ulipaji wa Mungu wa kisasi kunaongelewa kana kwamba ni kumlipa mtu ujira umfaao

kuanguka katika mikono

kupokea adhabu ya Mungu kunaongelewa kana kwamba mtu anaangukia katika mikono ya Mungu. Mikono" hapa inamaanisha uwezo wa Mungu wa kuhukumu.

Hebrews 10:32

siku zilizopita

"wakati uliopita"

baada ya kutiwa nuru

kujifunza kweli kunaongelewa kana kwamba Mungu aliwasha taa juu ya mtu. AT: "baada ya kujifunza ukweli kuhusu Kristo"

jinsi mlivyo vumilia mapingamizi makubwa

"ni jinsi gani umevumilia mateso mengi"

mlikuwa mmewekwa wazi katika dhihaka ya matukano na mateso

"Watu waliwadhihaki kwa matukano na mateso ya wazi wazi"

mlikuwa mmewekwa wazi katika dhihaka na matukano

watu waliwaasi ninyi na kukutukana wazi

mlikuwa mkishirkiana

"mlijiuna na wale"

urithi urio bora na wa milele

Baraka za Munguza milele zinaongelewa kana kwamba ni mali

Hebrews 10:35

Maelezo ya Jumla:

katika 10:37 ni nukuu kutoka kwa nabii Isaya katika Agano la Kale.

Msiutupe ujasiri wenu, ulio na zawadi kuu.

"Kukataa ahadi kunaongelewa kana kwamba ilikuwa ni kutupa kitu kisicho na thamani au kisicho na maana.

kwa kitambo kidogo

" kama Mungu alivyosema katika maandiko, kwa kila kitambo kidogo"

kwa muda kitambo sana

"mapema mno"

Hebrews 10:38

Maelezo ya Jumla:

katika 10:38 mwandishi ananukuu kutoka kwa nabii Habakuki, ambayo moja kwa moja inafuata nukuu kutoka kwa nabii Isaya 10:37.

mwenye haki wangu...kama akigeuka... pamoja naye

Haya maneno yanamaanisha kwa watu wa Mungu wowote.AT: "watu wangu waaminifu ...kama mmoja wao akigeuka...kwa mtu huyo" au " watu wangu waaminifu... kama wakigeuka ... nao"

kama akigeuka

kukosa ujasiri na imani kunaongelewa kana kwamba ilikuwa nikugeuka kutoka kufuata njia.

wanaogeuka kuelekea uangamivu

kukosa ujasiri na imani kunaongelewa kana kwamba ilikuwa ni kugeuka kutoka katika kufuata njia.

kwa kuzilinda imani roho zetu

kuishi milele na Mungu kunaongelewa kana kwamba ilikuwa ni kutunza roho ya mtu, Na roho hapa inamaanisha mtu mzima mzima.

Hebrews 11

Waebrania 11 Maelezo kwa jumla

Muundo

Mwandishi anaanza sura hii kwa kuelezea nini maana ya imani. Baadaye anapeana mifano mingi ya watu waliokuwa na imani na jinsi walivyoishi.

Dhana muhimu katika sura hii.

Imani

Katika maagano yote mapya na ya zamani, Mungu alihitaji imani. Watu wengine wa imani walifanya miujiza na walikuwa wenye nguvu sana. Watu wengine wa imani waliteseka sana.

<< | >>

Hebrews 11:1

Sentensi Unganishi:

Mwandishi anaongea vitu vtatu kuhusu imani katika maelekezo haya mafupi.

Sasa

Neno hili limetumika hapa kufanya kupumzika katika fundisho lake kuu. Hapa mwandishi anaanza kufafanua maana ya "imani."

Kwa hakika aliyo nayo mtu wakati atarajiapo

"imani ni msingi alionao mtu katika tegemeo"

hakika anatarajia

Hapa jambo hili hurejea katika ahadi za Mungu, hususani uhakika walionao waamini wote wa Yesu kuwa kunawakati watakuwa na Mungu mbinguni milele.

ambayo bado hayajaonekana

"yale ambayohatujayaona" au "ambayo hayajaonekana"

kwa sababu hii

"Kwa sababu kulikuwa na matukio ya hakika ambayo yalikuwa hayajatokea"

mababu walithibitishwa kwa imani yao

"Mungu aliwathibisha mababu zetu kwa sababu ya imani yao"

ulimwengu uliumbwa kwa amri ya Mungu

"Mungu aliimba dunia kwa kuiamuru iwepo"

kinachoonekana hakikuumbwa kwa vitu vinavyoonekana

"Mungu hakuumba tunavyoviona kutokana na vitu vinavyoonekana"

Hebrews 11:4

Sentensi Unganishi:

kisha mwandishi anatoa mifano mara nyingi kutoka Agano la Kale ya watu walioishi ka imani ingawa hawakupokea kile ambacho alikuwa amekiahidi wakati walipoishi duniani.

alishuhudiwa kuwa mwenye haki

'Mungu alishuhudia kwamba Habili alikuwa mwenye haki"

Abel bado anazungumza.

Yale aliyofanya Abel yanaendelea kutufundisha

alishuhudiwa kuwa mwenye haki

Mungu alimshuhudia kuwa mwenye haki"

Hebrews 11:5

Kwa imani Enoko alichukuliwa juu na hakuonja mauti

Kwa imani Enoko hakufa kwa sababu Mungu alimchukua.

Tazama Kifo

Kufa.

Kabla hajachukuliwa juu

"Kabla Mungu hajamchukua juu"

alikuwa ameshuhudiwa kwamba amempendeza Mungu. Maana dhaaniwa: 1) "Mungu alisema Enoki alikuwa amempendeza," 2) "Watu walisema Henoko alikuwa amempendeza Mungu."

sasa pasipo imani

Sasa hapa haimaanishi kwamba wakati huu lakini imetumika kuvuta usikivu kwa ajili ya kipengele kinachofuata.

Pasipo imani haiwezekani kumpendeza yeye

"mtu anaweza kumpendeza Mungu kama tu ana imani katika Mungu"

yeyote ajaye kwa Mungu

yeyote ajaye kwa Mungu

anayetaka kumwabudu Mungu na kuwa sehemu ya watu wake kunaongelewa kana kwamba ni kuja kwa Mungu. "mtu yeyote anayehitaji kuwa sehemu ya Mungu"

huwapatia zawadi

"huwapatia wale"

wale wote wamtafutao

Kujifunza kuhusu Mungu na kufanya juhudi kumtii kunaongelewa kana kwamba mtu anamtafuta mtu mwingine.

Hebrews 11:7

baad ya kupewa ujumbe wa kiungu

"Kwa sababu Mungu alimwambia yeye"

kuhusu vitu ambavyo havijaonekana

"kuhusu vitu ambavyo hapana hakuna hata mmoja amewahi kuviona kabla" au " kuhusu matukio ambayo hayajatokea bado"

Ulimwengu

Watu wanaoishi duniani wakati huo

akawa mrithi wa haki

Nuhu anaongelewa kana kwamba alikuwa akirithi mali ana utajiri kutoka kwa mwana familia. "alipokea kutoka kwa Mungu mwenye haki"

hivyo kulinganga na imani

"kwamba Mungu huwapa wale walio na imani katika yeye"

Hebrews 11:8

Alipoitwa

"pindi Mungu alipomwita"

alienda kwenye sehemu nje

"Aliacha nyummba yake kwenda kwenye sehemu"

Nchi ya ahadi

"Nchi ambayo Mungu alimuahidia.

aliishi katika nchi ya ahadi kama mgeni

"aliishi kama mgeni katika nchi ambayo Mungu alikuwa amemuahidi."

Warithi wenza

"warith pamoja." Hii inaongea kuhusu Abrahamu, Isaka, na Yakobo kana kwamba walikuwa warithi ambao wangepokea urithi kutoka kwa baba yao.

Mji ulio na misingi

Mungu anaongelewa kana kwamba ni mbunifu na mjenzi.

Mtaalam wa ujenzi

Mtu ambaye anaunda majengo.

mbunifu wa ujenzi

mtu anayebuni majengo

Hebrews 11:11

Uwezo wa kushika mimba

"Uwezo wa kuwa baba"

walimwona Mungu kuwa mwaminifu, ambaye aliwapa ahadi

"walimwamini Mungu, ambaye alikuwa amewaahidi vitu kuwa mwaninifu"

alikuwa karibia na kufa

"mzee sana kupata" au "mzee sana"

Wazao wasioweza kuhesabika... wengi kama nyota angani na mbegu za mchanga zisizohesabika kwenye ufukwe ambao hauhesabiki

Hii ilimuhusu Abrahamu kuwa na wana uzao mwingi sana.

ambayo haihesabiki

"ambayo mengi sana kuhesabu"

Hebrews 11:13

pasipo kupokea ahadi

"pasipo kupokea ahadiambazo Mungu alikuwa ameawaahidi

baada ya kuona na kuwasalimu kutoka mbali

"baada ya kujifunza kile Mungu atakachofanya wakati ujao"

walikiri

walitambua" au walipokea"

Walikuwa wageni na wapitaji katika nchi

"wageni" na "wapitaji" kimsingi yanamaanisha kitu kimoja. Hii inasisitiza kwamba nchi haikuwa nyumbani kwao kweli. Walikuwa wakisubiri kwa ajili ya nyumbani kwao kweli ambapo Mungu ametengeneza kwa ajili yao.

Nchi ya nyumbani.

"Nchi ambayo wanatokea"

Hebrews 11:15

wa mbinguni

"nchi ya kimbingu" au "nchi mbinguni"

Mungu haoni aibu kuitwa Mungu wao.

"Mungu anafurahi kuitwa Mungu wao" au "Mungu anajivuna kuwa Mungu wao"

Hebrews 11:17

alipojaribiwa

"pindi Mungu alipomjaribu"

kwake ambaye ilikuwa imesemwa

"kwake ambaye Mungu alisema"

Kutoka kwa Isaka uzao wako utaitwa

"Ni katika uzao wa Isaka amabao Mungu atafikiri uzao wako.

kuongea kwa mafumbo

namna ya kuongea." Hii ina maana kwamba mwandishi anachosema kisichukuliwe kama tukio ambalo linatokea kimwili. Mungu hakumleta Isaka kutoka kwa wafu.Lakini Abrahamu alikuwa anataka kumdhabihu Isaka wakati Mungu alipomzuia, ilikuwa kana kwamba Mungu alikmrudisha kutoka kwa wafu.

Alimpokea tena

"Abraham alimpokea Isaka tena

ilikuwa kutoka kwao

"ilikuwa kutoka kwa wafu

alimpokea

"Abrahamu alimpokea Isaka"

Hebrews 11:20

Yakobo aliabudu

"Yakobo alimwabudu Mungu"

Mwisho ulipokuwa umekaribia

"alipokuwa amekaribia kufa"

aliongeakuondoka kwa wana wa Israeli wangetoka Misri"

"aliongea wakati wana wa Israeli wangeondoka Misri"

wana wa Israeli

"wana wa Israeli" au " uzao wa Israeli"

aliwaelekeza kuhusu mifupa yake

Yusufu alikufa akiwa Misri. Aliwataka waru wake kuchukua mifupa yake wakati wataondoka Misri ili kwamba waizike mifuka katika nchi ambayo Mungu alikuwa amewaahidi.

Hebrews 11:23

Musa, alipozaliwa, alifichwa na wazazi wake kwa miezi mitatu

"Wazazi wa Musa walimfika kwa miezi mitatu baada ya kuzaliwa."

alikua

"Akawa mtu mzima

alikataa kuitwa

"aliwazuia watu kumuita"

Dharau zitokanazo na kumfuata Kristo

"udhoefu wa watu kutokumuheshimu kwa sababu alifanya kile ambacho Kristo angetaka"

Elekeza macho yake katika zawadi ya mbele

"Kufanya kile alichojua kuwa kitampatia zawadi huko mbinguni."

kumfuata Kristo

kumtii Kristo kunaongelewa kana kwamba walikuwa wakimfuata katika njia.

kuweka mach yake katika zawadi yake

Kufanya kile alichokifahamu kungemwezesha kupata taji mbinguni"

Hebrews 11:27

alivumilia kana kwamba alikuwa alimwona yeye asiye onekana

Musa anaongelewa kana kwamba alimwona Mungu, ambaye haonekani.

yule ambaye haonekani

"yeye ambaye hakuna mtu anaweza kumwona"

Kunyunyiza kwa damu

Hii inamaanisha amri ya Mungu kwa Waisraeli kuchinja mwana kondoo na kusambaza juu ya kila muimo wa kila nyumba mahali ambapo waliishi Hii ingezuia muharibifu kutowaaribu wazaliwa wao wa kwanza.

usiguse

"usidhuru" au " usiue"

Hebrews 11:29

Maelezo ya Jumla:

"wao" ya kwanza ina maanisha Waisraeli, na "wao" ya pili inamaanisha Wamisri na "wao" ya tatu inamaanisha kuta za Yeriko.

Walipita

Waisraeli walipita kupitia Bahari ya Shamu'

Walimezwa

"Maji yaliwameza Wamisri"

walimezwa

"Wamisri walizama ndani ya maji"

Walikuwa wamezunguka kwa siku saba

"Waisrael walitembea kwa kuzunguka kuta kwa siku saba"

Aliwapokea wapelelezi na kuwahifadhi salama

"Aliwaficha wapelelezi ili wawe salama

Hebrews 11:32

Sentensi Unganishi:

mwandishi anaendelea kuongelea kwa kile ambacho Mungu angefanya kwa mababu wa Israeli.

Niseme nini tena

Mwandishi anatumia swali kusisitiza kwamba kuna mifani mingi ambayo aliyoinukuu.

Muda hauta niruhusu

"Sita kuwa na muda wa kutosha"

Baraka

Jina la mtu.

ilikuwa ni kwa kupitia imani kwamba wali

"ilikuwa ni kwa ajili ya imani wale wanaume kama hivi"

walishinda

"waliwashinda watu wa falme ngeni"

Shinda

Iliyoshinda

Simamisha vinywa vya simba alizima nguvu ya moto... alikwepa makali ya ncha ya upanga

Njia ambazo watu wa Israeli waliokoka kutoka kifo. "Simba hawakuwala... moto haukuwaunguza." Upanga haukuwaua."

Waliponywa

"walipokea uponyaji kutoka kwa Mungu"

wakawa hodari katika vita, na wakashinda

"wakawa hodari katika vita na wakashinda"

Hebrews 11:35

Wanawake walipokea wafu wao tena kwa ufufuo

"Wanawake walipokea wafu waliokuwa wamekufa wakati Mungu alipowafufua"

Wengine waliteswa... wengine waliumizwa na dhihaka na vipigo... walipondwa mawe ... walikatwa kwa msumeno... walichinjwa

Wengine waliteseka wakati wengine wanadhihakiwa... na wakachapwa wengine walikufa kwa sababu ya kutupiwa mawe... wengine walikufa walipokatwa na misumeno... watu waliwaua

ufufuo ulio bora

Maana zinazo dhaaniwa 1) hawa watu watapata maisha bora mbinguni au 2)Watu hawa watapata ufufuo ulio bora zaidi ya wale wasio na imani.

wenginne walijaribiwa katika kutukana na kuchapwa... wapondwa mawe. walikatwa kwa wawili. waliuawa kwa upanga

watu waliwatukana na kuwapiga wengine... watu waliwaponda mawe.

wengine walijaribiwa katika kutukanwa, na hata minyororo na vifungo

Mungu aliwajaribu wengine kwa kuwaruhusu adui zao kuwa tukana na kuwachapa na hata kuwaweka vifungo"

katika mavazi ya kondoo na mbuzi

"wakiva tu ngozi za kondoo na mbuzi"

hawakuwa na makao

"hawakuwa na kitu" au " walikuwa masikini sana"

Ulimwengu haikuwastahili

"watu wa dunia hii haikuwastahili"

mapango, na ndani ya mashimo ya ardhi

"na wengine waliishi katika mapango na mashimo ya ardhi"

Hebrews 11:39

Ingawa watu hawa wote walikuwa wamehakikishwa na Mungukwa sababu ya imani yao, hawakupokea ahadi

"Mungu aliheshimu hawa kwa sababuya imani yao, lakini wenyewe hawakupokea kile ambacho Mungu alikuwa amekiahidi"

ahadi

"kile ambacho Mungu alikuwa amewaahidi."

ili kwamba pasipo yeye wasingeweza kukamilishwa

" ili kwamba Mungu angetukamikamilisha sisi na wao pamoja"

Hebrews 12

Waebrania 12 Maelezo kwa jumla

Muundo na mpangilio

Baada ya kuwafundisha watu umuhimu wa adhabu, mwandishi anaanza mfuatano ya mahubiri. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#exhort).

Watafsiri wengine wameweka kila msitari wa ushairi kulia kuliko maandishi mengine ili isomeke kwa urahisi. ULB inafanya hivi na ushairi katika 12:5-6, ambayo ni maneno kutoka Agano la Kale.

Dhana muhimu katika sura hii

Nidhamu

Mungu anataka watu wake kutenda yaliyo mema.Wakifanya kile hakipendi, anatakikana kuwarekebisha ama kuwadhibu. Yeye hufanya hivi jinsi baba wa duniani huwarekebisha na kuwadhibu watoto wao wanaowapenda. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#discipline)

<< | >>

Hebrews 12:1

Sentensi Unganishi:

Kwa sababu ya idadi kubwa ya waumini wa Agano la Kale, mwandishi anaongelea maisha ya imani ambayo waamini wanapswa kuishi na Yesu kama kielezo chao.

Maelezo ya Jumla:

inamaanisha mwandishi na wasomaji wake. Neno nyie linamaanisha wasomaji.

Tumezungukwa na kundi kubwa la mashahidi

" kundi kubwa la mashahidi linatuzunguka sisi" au "Kundi kubwa la mashahidi linasimama kama mfano kwetu."

Mashahidi

"Mashahidi" hapa inamaanisha waumini wa Agano la Kale katika sura ya 11 walioishi kabla ya shindano la imani ambayo waumini wanashindana sasa hivi.

tuweke kando kila mzigo na unatuzonga kwa urahisi

"mzito" hapana "dhambi inayozonga kwa urahisi" vinaongelewa kana kwamba mtu angeweza kuziondoa na kuzitua chini.

Mwanzilishi na mkamilishaji

"muumbaji na mkamilishaji." Hii inamaanisha kwamba Yesu ni chanzo imani ya waumini.Ndiye ambaye waumini wanamtumaini, na atahakikisha waumini wanafikia lengo lao.

furaha iliyowekwa mbele yake

Furaha ungetoka kwa Yesu kunaongelewa kana kwamba Mungu Baba aliyoiwekambele yake kufikia lengo.

aliidharau aibu yake

Hii inamaanisha hakujali kuhusu aibu ya ya kufa msalabani.

alikaa mkono wa kuume

"Mkono wa kuume" hapa unamaanisha sehemu ya heshima.

kiti cha enzi

"enzi" inamaanisha utawala wa Mungu kama mfalme.

kuchoka katika mioyo

"mioyo" inamaanisha mawazo ya mtu na hisia.

Hebrews 12:4

Hauateseka na dhambi vya kutosha kiasi cha kupoteza damu

"Umeshindana na dhambi, lakini wengine wamefanya hivyo kiasi cha kupoteza damu

dhambi, mdhambi, kutenda dhambi

Neno "dhambi" linamaanisha matendo, mawazo, na maneno ambayo yako kinyume na mapenzi na sheria za Mungu. Dhambi pia inaweza kumaanisha kutokufanya kitu ambacho Mungu anahitaji sisi tufanye.

damu

Neno "damu" linamaanisha kimiminikka chekundu ambacho kinatoka kwa mtu katika ngozi ya mtu wakati anapoumia au kidonda. Damu huleta virubtubisho vya uzima katika mwili wa mtu. Damu pia inamaanisha uzima na inapomwagika inaonyesha kifo. watu walipotengeneza dhabihu, waliua mnyama na kumwaga damu yake juu ya madhabahu. Na hii iliwakilisha dhabihu ya uhai wa wanyama kulipa kwa ajili ya dhambi za watu.

kutia moyo, utiaji moyo

Maneno kutia moyo na utiaji moyo inamaanisha kusema na kufanya vitu vinavyosababisha mtu kupata faraja, tumaini, ujasiri na moyo.

kulekeza, elekezo

Neno "kuelekeza" na "elekezo" yanamaanisha kutoa maalekezo ya moja kwa moja kuhusu nini kifanyike.

mwana, mwana wa

Neno "mwana" linamaanisha mvulama au mwanaume katika uhusiano na wazazi wake.Inaweza pia kumaanisha uzao wa mtu mme au kwa mtu mwana aliye asiliwa.

Bwana

Neno "Bwana" linamaanisha kwa mtu ambaye anaumiliki au uwezo juu ya watu. Inapotumika kwa herufi kubwa ni cheo kinachomaanisha Mungu.

huadhibu

Neno "adhibu" linamaanisha kufundiisha watu kutii maelekezo au kanuni kwa tabia njema.

upendo

kumpenda mtu mwingine in kumjali mtu huyo na na kufanya vitu vitakavyo mnufaisha. Kuna maana tofauti za upendo katika baadhi ya lugha inaweza konyeshwa kwa kutumia maneno tofauti: 1 Upendo utokao kwa Mungu kuna lengamazuri juu ya wengine hata kama kama haimnufaishi. Aina hii ya upendo unajali wengine bila kujali wanafanya nini. Mungu mwenyewe ni upendo na chanzo cha upendo wa kweli.

adhibu, adhabu

Neno adhibu maana ni kusababisha mtu kuteseka kwa sababu ya kukosea kwake.

Hebrews 12:7

Vumilia majaribu kama maonyo

"Elewa nyakati wa mateso Mungu hutufundisha nidhamu"

Mungu anashughulik na ninyi kama ashughulikavyo na wana

Hii inalinganisha unidhamishaji kwa Mungu kwa watu wake kama baba anavyo wanidhamisha watoto.

wana... mwana

Hiii ina jumuisha wamaume na wanawake, AT: "watoto... mtoto"

ni mtoto yupi ambaye baba yake hawezi kumrudi?

Mwandishi anatumia swali kuelewesha kwamba ni kawaida kwa kila baba mzuri kuwarudi watoto wake.

Lakini kama hakuna kurudiwa ambako sisi sote tunashiriki

"Hivyo kama haujapata kurudiwa na Mungu kama anavyowarudi wana wake wote"

basi ninyi ni haramu na sio wana wake

wale ambao Mungu hawarudi kunaongelewa kana kwamba ni wana ambao wamezaliwa na mwanamke na mwanaume ambao hawajaoana.

Hebrews 12:9

baba katika mwili

Neno "mwili" hapa linamaanisha mwanadamu.

kama warudiaji/ wanaotunidhamisha

wanao turudi

Je hatupaswi hata zaidi kumtii Baba wa kiroho na kuishi?

Mwandishi anatumia swali kusisitiza kwamba wangeweza kumtii Mungu Baba,

na ishi

"ili kwamba tuishi"

Baba wa roho

"Baba yetu wa kiroho" au Baba yetu wa mbinguni"

ili tushiriki utakatifu wake

"ili kwamba tuwe watakatifu kama Mungu alivyo mtakatifu"

tunda la amani

"Tunda" hapa ni alama na inaongelewa kana kwamba ni mtu aliye katika amani na ambaye alileta amani kwa wengine.

tunda la utauwa

Utauwa, ni hali ya mtu anaye mtii Mungu, inaongelewa kana kwamba ni tunda linakuwa juu ya mti. Mwandishi hapa anasema kwamba utauwa unaongezeka kama matokeo ya kurudiwa.

wale waliofundishwa nayo

"wale walio fundishwa kwa kurudiwa." Ambao Mungu amewafundisha kwa kuwarudi."

Hebrews 12:12

inueni mikono yenu iliyolegea na kufanya magoti yenu yaliyo dhaifu kuwa yenye nguvu. Nyosheni mapito ya nyayo zenu

Katika namna hii mwandishi anaongea kuhusu kuishi kama wakristo na kuwasaidia wengine.

njia iliyonyooka

Kuishi kama kumuheshimu na kumtukuza Mungu kunaongelewa kana kwamba ni kufuata njia iliyonyooka.

iliyo dhaifu haitapotoshwa

katika mfano huu wa kukimbia mashindanoni, "dahaifu" inawakilisha mtu mwingine katika shindano aliyeumia na anataka kuandoka katika shindano.Hili "geuka" linawakilisha wakristo wenyewe.

isipokuwa aponywe

"badala yake aimalike" au "badala yake Mungu atamponya"

Hebrews 12:14

Maelezo ya Jumla:

Esau, ambaye amesema katika maandishi ya Musa, inamaanisha kwa mwana wa kwanza wa Isaka na ndugu yake Yakobo.

tafuteni kuwa na amani na kila mmoja

" jaribu kuishi na kila mtu"

na pia ambao bila huo utakatifu hakuna atakayemwona Bwana

"na pia fanya bidii kuwa mtakatifu, kwa sababu ni watakatifu pekee ndio watakaomwona Mungu"

pia utakatifu

"pia tafuta utakatifu"

atakaye tengwa/ pungukiwa na neema ya Mungu

"hakuna mtu anapokea neema ya Mungu na kisha akaiachia" au " hakuna anaikataa neema baada ya kwanza kuamini katika yeye"

kwamba hakuna shina la uchungu litakalo kua na kusababisha shida ili kwamba wengi wasichafuliwe kwalo

kwamba hakuna yeyote anayekuwa kama mzizi mchungu, ambao unaweza kukua na kusababisha matatizo uharibifu kwa watu wengi"

alikataliwa

"baba yake, Isaka, alikataa kumbariki"

kwa sababu hakupata fursa ya kutubu

"kwa sababu haikuwa inawezekana kwa baba yake, Isaka, kubadilisha uamuzi wake"

ingawa alitafuta sana kwa machozi

Hapa aliyetafuta ni Esau

Hebrews 12:18

Sentensi Unganishi:

Mwandishi anakinzanisha katika waumini wakati wa Musa walipaswa kufanya chini ya sheria na kile ambacho waumini wa sasa wanapaswa kusihi baada ya kuja kwa Yesu chini ya agano jipya.

Maelezo ya Jumla:

Maneno haya "ninyi" "Nyie" inamaanisha waumini wa Kiebrania ambao mwandishi anawaandikia. Neno "wale" linamaanisha watu wa Israeli baada ya Musa kuwaongoza kutoka Misri. Nukuu ya kwanza inatoka katika maandishi ya Musa. Mungu anafunua katika ukurasa huu katika Waebrania kwamba Musa alisema alitetemeka alipoona mlima.

kwa kuwa hamkuja katika mlima ambao unaweaz kuguswa

kwa kuwa hamjafikia, kama watu wa Israeli walivyokuja, mlimani ambao unaweza kuguswa"

ambao unaweza kuguswa

Hii inamaanisha waumini katika Kristo hawajafikia mlima kama Mlima Sinai ambao mtu anaweza kugusa au kuona.

hamjafikia sauti ya tarumbeta

"Hamjafikia mahali ambapo palipo na mlio mkubwa wa tarumbeta"

au kwa maneno yatokanayo na sauti ambayo ilisababisha kila waisikiayo wasiombe neno lolote kusemwa kwao

"sauti" inamaanisha mtu anaye ongea. pale ambapo Mungu anaongea kwa namna ya kwamba wale waliosikia walimtaka asiongee neno jingine kwao"

kilichoamliwa

'kile ambacho Mungu aliamuru"

lazima apigwe kwa mawe

"ni lazima uiponde"

Hebrews 12:22

Maelezo ya Jumla:

Abeli alikuwa mwana wa mwanamme na mwanamke wa kwanza, Adamu na Eva. Pia Kaini mwana wao alimuua Habili.

Mlima Sayuni

Mwandishi anaongea Mlima Sayuni, hekalu la mlima Yerusalem kana kwamba lenyewe ilikuwa mbingu, nyumbani kwa Mungu.

Wamekuja

Wamewasili

Malaika elfu kumi

"Idadi isiyohesabika ya malaika"

mzaliwa wa kwanza

Hii inaongea waumini katika Kristo kana kwamba ni wana ambao ni wazaliwa wa kwanza. Hii inasisitiza sehemu yao maalumu na faida kama watu wa Mungu.

mmesajiliwa mbinguni

"ambao majina yao yameandikwa mbinguni

mpatanishi wa agano jipya

Hii inamaana Yesu alisababisha agano jipya kuwepo kati ya Mungu na wanadamu

Mmekamilishwa

"ambao Mungu amewafanya wakamilifu"

Damu ya kunyunyiza ambayo hunena zaidi kuliko damu ya Habili.

"Damu ya Yesu iliyonyunyizwa ambayo inamaana kubwa zaidi kuliko damu ya Habili, ambaye aliuawa na Kaini"

damu

damu hapa inasimama kwa kifo cha Yesu, kama damu ya Habili inavyoisimama kwa kifo chake.

Hebrews 12:25

Sentensi Unganish:

Baada ya kulinganisha uzoefu wa Waisraeli katika Mlima Sinai na uzoefu wa waumini baada ya Kristo kufa, mwandishi anawakumbusha waumini kwamba wana Mungu yuleyule anayewaonya leo. Hili ni onyo la tanzo kwa waumini.

Maelezo ya Jumla:

Hii nukuu inatoka kwa nabii Hagai katika Agano la Kale.

usije ukamkataa anayeongea

"msikilizeni anaye ongea.

kama hawakuepuka

"kama watu wa Israeli hakuepuka hukumu"

aliyewaonya duniani

Pengine 1) Musa aliye waonya duniani." au) Mungu aliyewaonya katika Mlima Sinai"

kama tukigeuka kutoka kwa yule anayetuonya

Kutmtii Mungu kunaongelewa kana kwamba mtu alikuwa akigeuka na kutoka kwake. "kama tusipomtii yeye anayeonya"

sauti yake iliitikisa ardhi

"Mungu alipoongea mlio wa sauti yake ilisababisha ardhi kutikisika"

ilitikiswa... tikisa

tumia neno ambalo tetemeko la ardhi inafanya katika kuitetemesha adrhi.

Hebrews 12:27

Maelezo ya Jumla:

Nukuu hii hapa kutoka kwa nabii Hagai inarudiwa kutoka mstari wa mwanzo.

kutoweshwa kwa vitu vile viteteshwavyo

'Mungu ataondoa vitu vyote vinavyotetemeshwa"

tetemeshwa

Tumia neno kwa tetemeko la ardhi linachofanya katika kutembea kwenye ardhi.

vilivyokwisha kuumbwa

"kwamba amekwisha umba."

hivi vitu ambavyo haviwezi

'vitu ambavyo havitetemeki"

kupokea ufalme

"kwa sababu tunapokea ufalme au " kwa "sababu Mungu anatufanya sisi kuwa wanafamilia wa ufalme wake"

tufurahi

"tumshukuru Mungu"

kunyenyekea katika kicho

"kunyenyekea" na "kicho" yana maanshabiliana maana na inasisitiza ukuu wa unyenyekevu kwa sababu ya Mungu"

Mungu wetu ni moto ulao

Mungu anaongelewa kana kwamba ni moto ambao unaweza kuchoma kitu chochote.

Hebrews 13

Waebrania 13: Maelezo kwa jumla

Muundo na mpangilio

Mwandishi anamalizia orodha ya mashauri aliyoyaanza katika sura ya 12. Halafu anawauliza wasomaji wake kumuombea anapomalizia barua hii.

Watafsiri wengine wametenga kila mistari wa ushairi kulia kuliko maandishi mengine ili isomeke kwa urahisi. ULB inafanya hivi na ushairi katika 13:6 ambayo ni maneno kutoka Agano la Kale.

Dhana muhimu katika sura hii

Ukarimu

Mungu anataka watu wake wakaribishe watu wengine kuja kwa nyumba zao kula chakula na hata kulala. Watu wake wanastahili wafanye hivi hata kama hafahamu vizuri watu wanaowaalika. Katika Agano la Kale, Abrahamu na binamu yake Lutu walionyesha ukarimu kwa watu ambao hawakuwafahamu. Abrahamu aliandaa chakula cha bei na Lutu akawakaribisha kulala kwake.Walikuja kufahamu baadaye kwamba watu hao walikua malaika.

__<< | __

Hebrews 13:1

Sentensi Unganishi:

katika kufunga sehemu hii, mwandishi anatoa maelekezo ya moja kwa moja kwa waumini namna wanapaswa kuishi.

Basi na upendo wa kindugu uendelee

"Endeleeni kuonyesha upendo wenu kwa waumini wengine kama mfanyavyo kwa mwana familia"

Usisahau

"hakikisha unakumbuka"

wakaribisheni wageni

"kuwaribisha wageni na kuwaonyesha wema"

Hebrews 13:3

kana kwamba mlikuwa mmefungwa pamoja

"kana kwamba mlikuwa gerezani pamoja nao"

Ndoa na iheshimiwe na watu wote na kila mmoja

"wanaume na wanawake walio na kuolewa waliolewa ni lazima waheshimiane.

kama miili yao ilitendewa kama wao

Hii inawatia moyo waumini kufikiri kuhusu mateso ya watu wengine kama ambaavyo wangeweza kufikiri juu ya mateso yao.

kitanda cha ndoa kiwe safi

Hii inamaanisha tendo la ndoa kana kwamba n kitanda cha watu walioana. AT: "wanaume na wanawakewaheshimu mahusiano ya ndoa yao na sio kwenda na watu wengine"

Hebrews 13:5

tabia zenu ziwe huru lakini sio katika kupenda fedha

"Msipende pesa"

Mtosheke

"Toshekeni"

Bwana ni msaidizi wangu...kunifanya mimi

Hii nukuu inatoka katika Zaburi ndani ya Agano la Kale.

Sitaogopa. Mwanadamu atanifanya nini?

Mwandishi anatumia swali kusisitiza kwamba haogopi watu kwa sababu Mungu anamsaidia.

Hebrews 13:7

tokeo la mwenendo wao

"matoke ya

kuiga imani yao

Tumaini katika Mungu na njia ya uzima iliyoongozwa na viongozi hawa inaongelewa kama "imani ya kweli'

ni yeye yule yule, leo, na milele

"Jana" hapa ina maana muda wote uliopita.

Hebrews 13:9

Maelezo ya Jumla:

Sehemu hii inamaanisha dhabihu ya wanyama walio wafanya waumini katika Mungu katika kipindi cha Agano Kale, ambayo inafunika dhambi zao kwa muda hadi kifo cha Yesu kilipokuja.

msije mkabebwa na mafundisho mageni mbalimbali

usisawichiwe kwa mafundisho mbalimbali kunaongelewa kana kwamba mtu alikuwa amechukuliwa kwa lazima.

moyo unapaswa kuimarishwa

"moyo" unasimama kwa ujasiri wa mtu, upendo, na ushupavu.

ni vizuri kwamba moyo ujengwe kwa neema, na siyo kwa vyakula ambavyo haviwasaidii wale wanao tembea kwa hivyo

"tunapata nguvu pale tunapofikilia jinsi Mungu ambavyo amekuwa mwema kwetu, lakini hatuwi na nguvu kwa kutii sheria za kuhusiana na chakula"

vyakula

Vyakula hapa vinasimama kuhusu sheria za chakula.

wale wanaotembea kwa hizo

Kuishi kunaongelewa kana kwamba ni kutembea.

madhabahu

madhabahu inasimama kwa sehemu ya ibada. Pia inasimama kwa ajili ya wanyama ambao makuhani katika dhabihu za agano la kale, ambavyo walichukua nyama kwa ajili yao na familia.

damu za wanyama zilizotolewa dhabihu kwa ajili ya dhambi inaletwa na kuhani mkuu sehemu takatifu

kuhani mkuu analeta ndani ya sehemu takatifu damu ya wanyama ambao makuhani waliwachinja kwa ajili ya dhambi.

wakati miili yao inachomwa moto

"wakati makuhani wanapochoma miili ya wanyama"

nje ya kambi

"mbali na mahali ambapo watu waliishi"

Hebrews 13:12

Sentensi Unganishi:

Kuna ulinganifu kati ya dhabihu ya Yesu na dhabihu za hekalu ya Agano la Kale.

Kwa hiyo

" Kwa njia hiyohiyo" au "Kwa sababu miili ya kujitoa iliunguzwa nje ya kambi"

nje yalango la mji

"Nje ya mji."

Kwa hiyo ngoja sasa twende

Kumtii Yesu kunaongelewa kana kwamba ni mtu alipaswa kuacha kambi kwenda nje Yesu alipo.

kubeba aibu yake

kutokuwa na huruma kunaongelewa kana kwamba in chombo ambacho kinapaswa kubebwa katika mikono ya mtu au juu ya mgongo wa mtu.

Hebrews 13:15

dhabihu ya sifa

Sifa inaongelewa kana kwamba ni dhabihu ya wanyama au uvumba.

sifa ambayo ni tunda la midomo ambayo inakiri jina lake

sifa inaongelewa kana kwamba ni tunda, na "midomo" inaongelewa kana kwamba ni miti inayozaa matunda. Kwa nyongeza "midomo" inawakilisha watu wakimsifu Mungu.

Jina lake

Jina la mtu linamwakilisha mtu.

tusisahau kufanya mazuri na kusaidiana

"mara zote tukumbuke kufanya mema na kusaidia wengine"

na dhabihu hiyo

Kufanya wema na kuwasaidia kunaongelewa kana kwamba ni dhabihu juu ya mimbari.

zitunzeni nafsi/roho zenu

roho za waumini,ambayo ni mwenendo wa maisha ya kiroho, yanaongelewa kana kwamba ni vyombo au wanyamaambao waangaliz wangeweza kutazama.

sio kwa huzuni

"huzunu" inasimama kama msiba au huzuni.

Hebrews 13:18

Sentensi Unganishi:

Mwandishi anafunga kwa baraka na salaamu

Tuombeeni

"Tuombeeni"hapa anamanisha mwandishi na wenzake.

tuna uhakika kwamba tuna dhamira njema/ safi

njema/ safi hapa inamaanisha hatuna hatia.

kwamba nitarudi tena kwenu hivi karibuni

Hii inaweza kusemwa katika mfumo tendaji. AT: "kwamba Mungu akipenda nitaondoa mambo yanayonizuia kuja kwenu"

Hebrews 13:20

Sasa

Hii ni sehemu ya mpya ya barua. Mwandishi hapa anamsifu Mungu na anatoa maombi ya mwisho kwa wasomaji wake.

mchungaji mkuu wa kondoo

Kristo katika jukumu lake la kiongozi na mlinzi wa wale wanaoaminikatika yeye kunaongelewa kana kwamba ni mchungaji wa kondoo.

kwa damu ya agano la milele

"Damu" hapa linasimama kwa kifo cha Yesu, ambacho ni msing kwa agano ambalo litakalodumu milele kati ya Mungu na waumini katika Kristo.

kuwakamilisha katika kufanya kila jambo jema ili kufanya mapenzi yake

"kuwakamilisha" hapa inamaanisha kuwafanya "kuweza" au "kuwafundisha"

afanye kazi ndani yetu

Neno hili "yetu" inamaanisha kwa mwandishi na wasomaji wake.

kwake uwe utukufu milele na milele

ambaye watu wote watamsifu milele

Hebrews 13:22

Sasa

Hii inaonyesha sehemu mpya ya barua. Hapa mwandishi anatoa maoni yake ya mwisho kwa wale anaowaandikia.

ndugu

Hii inamaanisha waumini wote anaowandikia wanume au wanawake.

huchukuliana na neno la kutia moyo

"kwa uvumilivu fikirini juu ya nilichokiandika kuwatieni moyo.

neno la faraja

"Neno" hapa linasimama kwa niaba ya ujumbe.

amewekwa huru

"hayuko tena gerezani"

Hebrews 13:24

wale wanaotoka Italia wawasalimu

Maana zinazodhaaniwa ni 1) mwandishi hayuko Italia, lakini kuna kundi la waumini waliotoka Italia walio pamoja naye au 2) mwandishi yuo Italia anapoandika barua hii.

Italia

Hili ni jina la sehemu wakati huo. Rumi ilikuwa mji mkuu wa Italia.

Utangulizi wa Yakobo

Sehemu ya 1: Utangulizi wa Jumla

Muhtasari wa Kitabu cha Yakobo

  1. Salamu (1:1)

  2. Kujaribiwa na ukomavu (1:2-18)

  3. Kusikia na kulitenda neno la Mungu

  4. Imani ya kweli inaonekana kwa matendo

  5. Matatizo katika jumuiya

  6. Mtazamo wa Mungu kuhusu maamuzi yako

  7. Maonyo ya kumalizia

Nani alikiandika kitabu cha Yakobo?

Mwandishi wa kitabu hiki anajitambulisha kama Yakobo. Kuna uwezekano Yakobo alikuwa ndugu wa kambo wa Yesu. Yakobo alikuwa kiongozi wa kanisa la mwanzo na mwanachama wa baraza la Yerusalemu. Mtume Paulo pia alimuita "mhimili" wa kanisa.

Huyu siye mtume Yakobo. Mtume Yakobo aliuwawa kabla ya barua hii haijaandikwa.

Kitabu cha Yakobo kinahusu nini?

Katika barua hii Yakobo anawapa moyo waumini waliokuwa wanateseka. Aliwaeleza kwamba Mungu hutumia mateso kuwafanya wawe Wakristo wakomavu. Yakobo pia anawaelezea umuhimu wa waumini kutenda mema. Aliandika mengi kuhusu jinsi waumini wanapaswa kuishi na kuwatendea wengine. Kwa mfano aliwaamuru watendeane haki, kutopigana na kutumia mali kwa hekima.

Yakobo aliwafunza wasomaji wake kutumia mifano mingi kutoka kwa mazingira. Kwa mfano katika 1:6, 11 na 3:1-12. Pia sehemu nyingi za barua hii zinafanana na yale Yesu aliandika kwenye Hotuba mlimani (Mathayo 5-7).

Akina nani walikuwa "Makabila kumi na mbili yaliyotawanyika?"

Yakobo alisema alikuwa anawaandikia "makabila kumi na mbili yaliyotawanyika"(1:1) Wasomi wengine wanafikiri kwamba Yakobo aliwaandikia Wakristo Wayahudi. Wasomi wengine wanafikiri kwamba Yakobo aliwaanndikia Wakristo wote kwa ujumla. Barua hii ni mojayapo ya "barua za jumla" kwa vile haikuandikiwa kanisa fulani ama mtu fulani.

Kichwa cha Kitabu hiki kitafsiriwe namuna gani?

Watafsiri wanaweza kukiita kitabu hiki kutumia kichwa chake cha asili "Yakobo" ama wanaweza kuchagua kichwa kinachoeleweka zaidi kama "Barua kutoka kwa Yakobo" ama "Barua iliyoandikwa na Yakobo" (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-names)

Sehemu ya 2: Dhana muhimu za kidini na kitamatudi

Je, Yakobo alitofautiana na Paulo kuhusu jinsi ya mtu kuhesabiwa haki mbele za Mungu?

Paulo alifundisha kwamba Wakristo wanahesabiwa haki kwa imani na siyo kwa vitendo. Inaonekana Yakobo anawafundisha Wakristo kwamba Wakristo wanahesabiwa haki kwa vitendo vyao. Hali hii inaweza kutatanisha. Lakini kuelewa kuzuri kuhusu kile Paulo na Yakobo walifundisha kunaonyesha kwamba hawakutofautiana. Wote walifundisha kwamba mtu anahitaji imani "ili ahesabiwa haki. Wote walifundisha pia kwamba imani ya kweli itamfanya mtu kutenda mema. Paulo na Yakobo waliyafundisha mambo haya kwa njia tofauti kwa sababu walikuwa na hadhira tofauti zilizotaka kujua vitu vingi kuhusu kuhesbiwa haki. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#justice and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#works)

Sehemu ya 3: Maswala muhimu ya tafsiri

Watafsiri wanatakiwa kuashiria namna gani mipito kati ya mada za kitabu cha Yakobo?

Barua hii inabadilisha mada haraka. Wakati mwingine Yakobo hawaelezi wasomaji kwamba karibu anabadilisha mada. Inakubalika kuacha mistari kuonekana haina uhusiano. Ni busara kuweka kando aya kwa kuanzisha mistari mipya ama kuacha nafasi katikati ya mada.

Ni maswala gani muhimu katika maandishi ya kitabu cha Yakobo?

(See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/Translate.html#translate-textvariants)

James 1

Yakobo 01 Maelezo kwa jumla

Dhana muhimu katika sura hii

Majaribio na vishawishi

Maneno haya mawili yanatokea pamoja katika (Yakobo: 1:12-13) Maneno yote "yanasema juu ya mtu anayeweza kuchagua kutenda mazuri na kutenda mabaya. Tofauti yao ni muhimu. Mungu anamjaribu mtu na anahitaji atende mema. Shetani anamshawishi mtu huyo na anataka atende maovu.

Mataji

Taji ambalo mtu hupewa baada ya kuyashinda majaribio ni tuzo. Hiki ni kitu amabaco watu wafanyacho kitu kizuri hupokea. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#reward)

Mifano muhimu za usemi katika sura hii

MIfano

Yakobo anatumia mifano nyingi na "unastahili kuelewa maswala yaliyo kwenye https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor kabla ya kuzitafsiri vizuri.

Maswala mengine ya utata katika tafsiri ya sura hii

"Kwa Makabila kumi na mbili yaliyotawanyika"

Haikuwa wazi kama Yakobo aliwaandikia wa nani katika barua hii.Anajiita mwenyewe kama mtumishi wa Bwana Yesu Kristo, na kwa hivyo kuna uwezekano alikuwa akiwaandikia Wakristo. Lakini anawaita wasomaji wake "Makabila kumi na mbili yaliyotawanyika", maneno yatumikayo kuashiria Wayahudi. Kuna uwezekano ametumia maneno hayo kama mfano ya "wengi ambao Mungu amewachagua" ama aliandika barua hii wakati Wakristo wote walikuwa wamekomaa kama Wayahudi.

| >>

James 1:1

Sentensi unganishi

Baada ya salam zake za ufunguzi, Yakobo anawaambia waamini kwamba kusudi la majaribu ni kupima imani.

Yakobo, mtumishi wa Mungu na Bwana Yesu Kristo.

Neno "Niko" linamaanisha " Mimi, Yakobo ni mtumishi wa Mungu na Bwna Yesu Kristo"

Yakobo

Yakobo alikuwa ndugu yake na Yesu.

Kwa kabila kumi na mbili waliotawanyika.

Hii inaelezea eidha wayahudi wote wa Kikiristo waishio nje ya Israeli au Wakristo wote waishio popote duniani.

Makabila kumi na mbili.

Neno "makabila "kumi na mbili" yanamaanisha watu wote wa Israeli kwa kuwa waligawanywa katika makabila "kumi na mbili". Kwenye mistari hii makabila kumi na mbili yanamaanisha Wayahudi wote wa Kikristo au Wakristo wote duniani. Hapa neno "kumi na mbili" hutumika kama jina na namba "kumi na mbili" inapaswa kuandikwa kama neno sio kama namba.

Kutawanyika

Neno "kutawanyika" kunamaanisha Wayahudi wote waliotawanyika kwenye nchi nyingine mbali na nyumbani kwao Israeli. Kenye mistari hii "kutawanyika" linamaanisha Wakristo wa kiyahudi waishio nje ya Israeli au Wakristo wote waliopo popote duniani.

Salam

Salam ya kawaida kama "habari" au "siku njema".

Furahini ndugu zangu, mpatapo matatizo.

"Waamini wenzangu, yaone matatizo yote uliyonayo kama mambo ya kukufanya ushangilie"

Jaribu la imani yenu inatengeneza uvumilivu.

Maneno "jaribu", "imani yenu", na "kuvumilia" ni maneno yanayosimama kuonyesha matendo. Mungu hutujaribu ili kujua ni kwa namna gani tunamwamini yeye na kumtii. Waamini ("ninyi") mwamini yeye na mvumilie mateso. "Mnapokutana na magumu Mungu anagundua ni kwa kiasi gani unamwamini. Na matokeo yake unakuwa na uwezo wa kushinda majaribu magumu zaidi.

James 1:4

Tuache uvumilivu ukamilishe kazi yake.

Hapa uvumilivu imezungumzwa kama vile mtu yupo kazini. "Jifunze kuvumilia magumu yote"

Kukua kabisa

Kuwa na uwezo wa kumwamini Kristo na kumtii yeye katika hali zote.

Usipungukiwe chochote

Hii inaweza kuwa sentensi chanya "kuwa na uwezo kumtii Mungu kwa kila jambo"

Muombe Mungu, yeye atoaye

"Muombe Mungu. Ni yeye atoaye"

Ukarimu na "bila kukemea

Hii inaweza kuzungumziwa kwa mtazamo chanya "ukarimu au furaha"

Atawapa

"Mungu atawapa" au "Mungu atajibu maombi yenu"

James 1:6

Kwa imani, bila mashaka yoyote

Hii inaweza kuzungumziwa kwa mtazamo chanya. "Kwa uhakika zaidi kuwa Mungu atajibu"

Kwa yeyote mwenye mashaka ni kama mawimbi ya bahari yanavyoendeshwa na upepo na kuchafuka kwa bahari

Yeyote mwenye mashaka kuwa Mungu atamsaidia ni kama maji ndani ya bahari au maziwa makubwa yanayopita katika uelekeo tofauti.

Ana nia mbili

Nia. Neno "nia mbili" linamaanisha mawazo ya mtu pale anaposhindwa kufanya maamuzi. "Anashindwa kuamua amfuate Yesu as la"

Hana msimamo kwenye njia zake zote

Hapa anazungumziwa mtu amabye hawezi kukaa kwenye njia moja badala yake anaenda njia moja baada ya nyingine.

James 1:9

Ndugu masikini

"mwamini asiye na pesa nyingi"

Kujivuna kwa cheo chake cha juu

Mtu ambaye Mungu anembariki anazungumza kama vile amesimama mahali pa juu sana.

Lakini tajiri

"lakini mtu aliye na pesa nyingi." Maana nyingine ni 1) huyu mtu tajiri ni mwamini, au 2) huyu mtu tajiri si mwamini.

Wa cheo cha chini

Mwamini tajiri anapaswa kufurahi kwamba Mungu ameyaruhusu mateso. "anapaswa kuwa na furaha kwamba Mungu amempa nafsi hiyo"

Atapita kama ua la porini kwenye majani

Matajiri wanafananishwa na maua ya porini ambayo yanakuwa hai kwa mda mfupi.

Mtu tajiri atachakaa katikati ya safari zao

Kama ambavyo maua hayafi ghafla lakini yanachakaa kwa mda mfupi , pia matajiri hawatakufa ghafla lakini watachukua mda mfupi kupotea.

Katikati ya kazi yake.

Shughuli za kila siku za tajiri zinazungumzwa kama safari aliyokuwa anaifanya. Hii inaelezea namna ambavyo hakufikiri chochote juu ya kifo chake hapo baadae na hivyo kitakuja ghafla.

James 1:12

Sentensi unganishi.

Yakobo anawakumbusha waamini wanaosema Mungu hasababishi majaribu; anawaambia namna ya kukabiliana na majaribu.

Baraka

Bahati, vizuri.

Kuvumilia majaribu

Kuendelea kuwa mwaminifu kwa Mungu uwapo katika magumu.

Kushinda majaribu

Amethibitishwa na Mungu.

Kupokea taji ya uzima

Uzima wa milele unazungumziwa kama taji ya maua inayowekwa kwenye kichwa cha washindi. "pokea uzima wa milele kama tuzo"

Imeahidiwa kwa wale wanaompenda Mungu.

Hii imeelezewa katika hali ya utendaji "Mungu aliahidi taji ya uzima kwa wale wampendao"

Anapojaribiwa

"Anapotamani kufanya uovu"

Nimejaribiwa na Mungu

Hii imeelezewa katika hali ya utendaji. "Mungu amesababisha nifanye maovu"

Mungu hajaribiwi na uovu

Hii imeelezewa katika hali ya utendaji. "Mungu hatamani kufanya lolote ovu"

Wala mwenyewe hamjaribu yeyote

"Na Mungu mwnyewe hamsababishi mtu kufanya uovu"

James 1:14

Kila mtu anajaribiwa na tamaa zake mwenyewe

Tamaa za mtu zinazungumzwa kama vile mtu mwingine ameshawishi afanye dhambi.

Zinamshawishi na kumvuta mbali

Tamaa mbaya zinaendelea kuzungumzwa kama mtu anavyoweza kumshawishi mwingine.

Kushawishi

kuvutia, kumshawishi mtu kufanya uovu.

Ndipo baada ya tamaa ya dhambi kubeba mimba, dhambi huzaliwa, na baada ya dhambi kukomaa sawasawa, huishia katika mauti.

Tamaa inaendelea kuzungumzwa kama mtu, na hapa inaelezewa wazi kama mwanamke mwenye mimba ya mtoto. mtoto anaelezewa kama dhambi. Thambi ni mtoto mwingine wa kike ambaye anakuwa na kupata mimba naanazaa kifo. Mtiririko huu ni picha inayoonyesha namna ambavyo mtu atakufa kiroho na kimwili kwa sababu ya tamaa zake mbaya na dhambi.

Msidanganyike

"Msiache mtu yeyote awadanganye" au "msijidanganye wenyewe"

James 1:17

Kila zawadi iliyo nzuri na kila zawadi iliyokamilika

Sentensi hizi mbili zina maana moja. Yakobo alizitumia kusisitiza kuwa kila kizuri alichonacho mtu kinatoka kwa Mungu.

Baba wa nuru.

Mungu, muumbaji wa nuru zote zilizopo juu angani (jua, mwezi na nyota) inajulikana kuwa ni Baba yao.

Kamwe habadiliki kama kivuli kibadilikavyo

Hii inamuelezea Mungu kama mwanga usiobadilika tofauti na jua, mwezi, sayari na nyota ambazo zinapita katikati ya anga na zinabadilisha nuru yake. "Mungu habadiliki kama jua, mwezi na nyota ambazo zinatokea na kupotea"

Kutupa sisi

Neno "sisi" linamaanisha Yakobo na hadhira yake.

Katupa uzima

Mungu aliyetupa uzima wa milele anazungumziwa kana kwamba ametupa uzima.

Neno la kweli

Ujumbe wa kweli wa Mungu.

Kama uzao wa kwanza

Yakobo anatumia utamaduni wa Kiebrania wa zao la kwanza kama njia ya kuelezea thamani ya Mwamini wa Kikristo kwa Mungu. anaelezea kuwa kutakuwa na waamini wengi sana baadae.

James 1:19

Mnajua hili

Yaweza kumaanisha 1) "mnajua hili" kama amri, kuwa makini juu ya lile ninalotaka kuwaandikia au 2) "mnajua hili" kama sentensi kwamba ninataka kuwakumbusha juu ya jambo ambalo mnalijua.

Kila mmoja anapaswa kuwa mwepesi wa kusikia, siyo mwepesi wa kuongea

Watu wanapaswa kusikiliza kwa makini na kuzingatia maneno haya " usiwe mwepesi kuongea" haimaanishi uongee taratibu.

si mwepesi wa hasira

"usishikwe na hasira mapema"

hasira ya mwanadamu haiwezi kutenda haki ya Mungu

Mtu anapokuwa na hasira hawezi kufanya kazi ya Mungu, ambayo ni haki.

wekeni mbali uchafu wa dhambi na ubaya wote

Dhambi na ubaya vimezungumzwa hapa kama vitu ambavyo vinapaswa kuwekwa mbali au kutupwa.

wekeni mbali uchafu wa dhambi na ubaya wote

Hapa uchafu wa dhambi na ubaya vinamaanisha kitu kimoja. Yakobo ameyatumia kusisitiza ni kwa jinsi gani dhambi ilivyo mbaya. "Acheni kufanya aina zote za dhambi"

uchafu wa dhambi

Hapa uchafu inamaanisha dhambi na ubaya.

Kwa unyenyekevu

"Bila kujivuna" au "bila kiburi"

lipokeeni neno lililopandwa

Neno "kupanda" linamaandishwa kuweka kitu flani ndani ya kitu kingine. Hapa neno la Mungu limetumika kama mmea ambao unapaswa kukua ndani ya waamini. "Utii ujumbe wa Mungu aliousema kwako"

lipokeeni neno lililopandwa

"Neno" linamaanisha neno la Mungu linalosimama kama ujumbe wa ukombozi ndani ya Yesu Kristo ambapo Mungu anawaambia waamini. Wakiliamini, Mungu atawaokoa.

kuokoa roho zenu

"Awaokoe ninyi toka kwenye hukumu ya Mungu"

roho

Hapa neno "roho" inamaanisha mtu.

James 1:22

Litiini neno

Wanapaswa kutii amri zilizoamriwa na Mungu.

Mkijidanganya wenyewe

"mnajidanganya wenyewe

Kwa kuwa kama yeyote alisikiaye neno bila kulitendea kazi ni sawa na mtu ajiangaliaye uso wake halisi katika kioo.

Mtu anayesikiliza maneno ya Mungu lakini hayatii anafananishwa na mtu anayejiangalia kwenye kioo na baadae anasahau muonekano wake.

uso wake halisi

Uso wake kama ulivyo.

Hujitathmini uso wake na baada ya mda mfupi husahau

Mtu anayejiangalia uso wake na baadae akasahau muonekano wake ni sawa na mtu aliyesikia neno la Mungu na kusahau alichosikia.

mtu yule anayeiangalia kwa uangalifu sheria kamili.

Hii inaendelea kuelezea picha ya sheria kama kioo.

Sheria kamili ya uhuru

"sheria kamili inayoruhusu watu kuwa huru"

Mtu huyu atabarikiwa katika utendaji wake.

Hii inaweza kuelezewa katika hali ya kutenda "Mungu atambariki huyu mtu kama akiitii sheria"

James 1:26

kujiona mwenyewe kuwa mtu wa dini

"Anadhani anamuabudu Mungu kwa usahihi

Ulimi wake

Kuudhibiti ulimi wa mtu inamaanisha kudhibiti kauli zake.

udanganyifu

"mjinga" au "kupotosha"

Moyo wake

Hapa moyo inamaanisha imani yake au mtazamo wake.

Dini yake ni bure

"Anamuabudu Mungu bure"

Safi na isiyoharibiwa

Yakobo anaizungumzia dini , namna watu wanavyomuabudu Mungu kama kitu amabacho ni safi na kisichoharibiwa. Hii ni utamaduni wa Kiyahudi kuelezea namna ambavyo kitu kimekubalika na Mungu. "kukubalika kabisa"

mbele za Mungu wetu na Baba

Anaelezewa Mungu.

Yatima

Yatima

Wajane katika mateso yao

Wanawake wanaoteseka kwa sababu waume zao wamefariki.

Kujilinda na ufisadi wa dunia

Kutokubali uovu wa dunia hii ukakusababisha ukatenda dhambi

James 2

Yakobo 02 Maelezo ya Jumla

Dhana muhimu katika sura hii

Mapendeleo

Wasomaji wengine wa Yakobo waliwatendea matajiri na wenye uwezo mazuri na kuwatendea maskini vibaya. Haya ndiyo mapendeleo na Yakobo anawaambia kwamba hii ni mbaya. Mungu anataka maskini kwa matajiri watendewe wema.

Kuhesabiwa haki

Kuhesabiwa haki ni kile hufanyika wakati Mungu anamfanya mtu kuwa mwenye haki.Yakobo anasema Mungu huwafanya wenye haki ama huwahesabu wenye haki watu ambao imani yao huendana na matendo mazuri. (tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#justice na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith)

Maswala mengine ya utata katika tafsiri ya sura hii

Alama za nukuu

Maneno "Nionyeshe imani yako bila matendo na nitakuonyesha imani yangu kwa matendo" ni magumu kuelewa. Watu wengine hufikiri ni yale "wengine wagesema" kama maneno yaliyo na alama za nukuu. Matoleo mengi huyatafsiri kama maneno Yakobo anamwelezea "mtu huyo".

"Wewe una..." "Mimi nina..."

Watu wengine hufikiria kwamba maneno "wewe" na "mimi" yametumiwa kumaanisha "baathi ya watu" na "waatu wengine". Iwapo ni sahihi mstari wa 18 unaweza tafsiriwa , "Watu wengine wanaweza sema, "Watu wengine wana imani na baadhi ya watu wana matendo, siyo watu wote wana zote."Iwapo sentensi ifuatayo pia ni yenye watu wangesema," inaweza tafsiriwa "Baadhi ya Watu wanaonyesha imani yao bila matendo na watu wengine wanaonyesha imani yao kwa matendo. Wote wana imani." Katika hali zote mbili, msomaji ataelewa tu ukiongezea sentensi ya ziada. Ni vyema kutafsiri jinsi ULB hufanya. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metonymy and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

<< | >>

James 2:1

Sentensi unganishi:

Yakobo anaendelea kuwaambia waamini wa Kiyahudi waliotawanyika namna ya kuishi kwa kupendana na kuwakumbusha kutowapendelea matajiri juu ya masikini.

Ndugu zangu

Yakobo anawaandikia ndugu zake ambao ni waamini wa Kiyahudi . "waamini wenzangu" au "ndugu zangu katika Kristo"

Ishikeni imani ya Bwana Yesu Kristo

Mwamini Yesu Kristo.

Bwana wetu Yesu Kristo

Neno "wetu" linamaanisha Yakobo na waamini wenzake.

upendeleo kwa watu wengine

shauku ya kumsaidia mtu fulani zaidi ya mwingine

Kama mtu fulani

Yakobo anaanza kuelezea hali ambayo waamini wanamthamini sana tajiri kuliko masikini.

amevaa pete za dhahabu na mavazi mazuri

"amevaa kama mtu tajiri"

keti hapa mahali pazuri

"keti hapa sehemu ya heshima"

simama pale

"hamia sehemu isiyo na heshima"

Kaa chini ya miguu yangu

Hamia sehemu ya kunyenyekea

Je, hamuhukumiani ninyi wenyewe, na kuwa waamuzi wenye mawazo mabaya?

Yakobo alitumia swali kuwakemea wasomaji wake. "Mnahukumiana wenyewe kwa wenyewe na kufanya maamuzi mkiwa na mawazo mabaya"

James 2:5

Sikilizeni, ndugu zangu wapendwa

Yakobo anawachukulia wasomaji wake kama ndugu. "kuweni makini, ndugu zangu wapendwa"

Mungu hakuwachagua ... wampendao?

Yakobo anatumia swali kuwafundisha wasomaji wake wasiwe na upendeleo. "Mungu aliwachagua ... mpende yeye"

masikini

"watu masikini."

Kuwa tajiri katika imani

Kuwa na imani kubwa ni utajiri. "kuwa na imani thabiti kwa Kristo"

Warithi

Watu ambao Mungu aliwaahidi watairithi mali na utajiri kama vile watu warithipo toka kwa ndugu wa familia.

Lakini ninyi

Yakobo anaongea na hadhira yote.

mmewadharau masikini

"Mmewadhalilisha masikini"

Je, sio matajiri wanaowatesa ninyi

Hapa Yakobo anatumia maswali kuwasahihisha wasomaji wake. "Ni matajiri wanaowatesa ninyi."

tajiri

"watu matajiri"

wanaowatesa

"wanaowatendea mabaya"

Sio wao ... mahakamani?

Hapa Yakobo anatumia maswali kuwasahihisha wasomaji wake. " matajiri ndio wao ... mahakamani."

wanaowaburuza mahakamani

"wanaowapeleka kwa nguvu mahakamani na kuwashitaki kwa hakimu"

Hawalitukani ... mnaitiwa?

Hapa Yakobo anatumia swali kurekebisha na kufundisha wasomaji wake. "Matajiri ... mnaitiwa?

Jina zuri

"jina la Kristo" hii ni njia moja wapo ya kuelezea jina la Yesu. "Kristo ambalo kwalo mnaitiwa"

mnaitiwa

"mnajulikana kwalo"

James 2:8

ninyi mkiitimiza

Neno "ninyi" inamaanisha waamini wa Kiyahudi.

kutimiza sheria ya kifalme

"kutii sheria za Mungu." Mungu alitupa sheria za Musa zilizorekodiwa katika agano la kale.

Utampenda jirani yako kama wewe mwenyewe

Yakobo ananukuu maneno toka kitabu cha mambo ya walawi.

Jirani yako

"watu wote"au "kila mtu"

mwafanya vyema

"mnafanya vyema" au "mnafanya yaliyo sahihi"

Kama mkipendelae

"kutoa huduma ya kipekee" au "kutoa heshima kwa"

kutenda dhambi

"kutenda dhambi" ni kuvunja sheria.

mtahukumiwa kwa shiria kama wavunja sheria.

"mna makosa ya kuvunja sheria"

James 2:10

Kwa kuwa yeyote atiiye

"Yeyoye anayetii"

bado akajikwaa ... sheria yote

Kujikwaa ni kuanguka chini wakati mtu anatembea. kutotii sheria ni sawa na kujikwaa wakati wa kutembea.

katika nukta moja

kwa sababu ya kutotii kwa sheria moja tuu

Kwa kuwa Mungu aliyesema

Hii inamuelezea Mungu aliyempa sheria Musa.

usifanye

"kufanya" ni kuchukua hatua

Kama ninyi .... lakini una ... ume

"ninyi" inamaanisha "kati yenu" Japokuwa Yakobo aliwaandikia waamini wengi wa Kiyahudi kwenye sehemu hii ametumia umoja kama vile alikuwa amzungumzia mtu mmoja.

James 2:12

Kwa hiyo zungumzeni na kutii

"hivyo mnatakiwa muongee na kufanya" Yakobo aliwaamuru watu kufanya hivi.

mko karibu kuhukumiwa na sheria ya uhuru.

"Mungu atawahukumu lwa sheria ya uhuru"

Kwa sheria

Mungu atawahukumu kulingana na sheria

Sheria ya uhuru

"Sheia inayotoa uhuru wa kweli"

Huruma hujitukuza juu

"Huruma ni bora kuliko" au "huruma inashinda" Hapa huruma na haki vimezungumwa kama vile ni mtu.

James 2:14

Sentensi unganishi

Yakobo anawatia moyo waamini waliotawanyika kuonyesha imani yao mbele za watu. Kama vile Abrahamu alivyoionesha imani yake kwa vitendo.

Kuna uzuri gani, ndugu zangu, kama mtu anasema ninayo imani, lakini hana matendo?

Yakobo anatumia swali kuifundisha hadhira yake. "Waamini wenzanhu, sio vizuri kabisa mtu akisema ana imani lakini hana matendo."

anayo imani

Yakobo anazungumzia imani, kumuamini Mungu.

haina matendo

Yakobo anazungumzia matendo kuwa ni kufanya matendo mema.

Je, imani hiyo yaweza kumwokoa?

Yakobo anazungumzia imani kuwa kumuamini Mungu kuna nguvu ya pekee katika kumuokoa mwanadamu lakini Imani haitoshi. "Imani hiyo haiwezi kumuokoa."

kumuokoa

"Kumuokoa toka kwenye hukumu ya Mungu."

mkaote moto

"kuwa na nguo za kutosha kuvaa" au "kuwa na sehemu ya kulala."

mle vizuri

"kuwa na chakula cha kutosha."

ya mwili

kula, kuvaa na kuishi vizuri.

yafaa nini?

Yakobo anatumia swali hili kuifundisha hadhira. "hivi sio vizuri."

wa kiume na wa kike

Waamini wenzangu katika Yesu, wanaume kwa wanawake

imani ... imekufa

Yakobo anaizungumzia imani kuwa ni hai mtu afanyapo matendo mema na imekufa kama mtu hatafanya matendo mema.

imani ... ina matendo

Imani inaambatana na mtu afanyaye matendo mema.

James 2:18

Bado mtu fulani anaweza kusema

Yakobo alikuwa anasahihisha uelewa wa hadhira yake juu ya imani na matendo.

Una imani, na mimi ninayo matendo

"Inakubalika iwapo mtu mmoja ana imani na mwingine ana matendo." Yakobo anaelezea ni kwa namna gani watu wnaweza kulumbana dhidi ya mafundisho yake.

Una imani, na mimi ninayo matendo ... nionyeshe imani yako

Yakobo anazungumzia imani na matendo kama vitu ambavyo watu wanaweza kuwa navyo na kuwaonesha wengine.

nitakuonyesha imani yangu kwa matendo yangu

Yakobo anazungumza kuwa imani inaweza kuonekana endapo mtu atafanya matendo mema. "Nitaionesha imani yangu kwa kufanya matendo mema"

mapepo nayo yanaamini hivyo na kutetemeka.

"mapepo nayo yanaamini, lakini yanaogopa kwa hofu. Yakobo anafananisha mapepo na watu wanaosema wana imani lakini hawafanyi matendo mema. Yakobo anasema pepo wana busara maana wanamuogopa Mungu wakati watu hawamuogopi.

Je, unataka kujua, ewe mtu mpumbavu, namna ambavyo imani hiyo pasipo matendo isivyofaa?

Yakobo alitumia swali kuwakemea watu ambao hawakumsikiliza. "Ewe mpumbavu, hautaki kunisikiliza thibitisha namna isivyofaa imani bila matendo.

Je, unataka kujua ... isivyofaa?

"Nitawaonyesha ni jinsi gani ... isivyofaa."

James 2:21

Maelezo ya jumla

Kwa kuwa kulikuwa na waamini wa Kiyahudi walijua habari za Abrahamu ambaye waliambiwa na Mungu zamani.

Je, si baba yetu Abrahamu alihesabiwa haki

Hili ni swali linalotumika kuwakemea wapumbavu walioelezewa toka 2:18 waliokataa kuamini kuwa imani na matendo vinaenda sambamba." Abrahamu baba yenu alihesabiwa haki."

haki kwa matendo

"haki kwa kufanya matendo mema"

Baba

"baba" imetumika kama "mababu"

Mnaona

Neno "wewe" linamaanisha umoja. Yakobo anaongea na hadhira yake kama anaongea na mtu mmoja.

mnaona

kuona inaweza kumaanisha "kuelewa"

imani yake ilifanya kazi na matendo yake

Yakobo anazungumzia imani inafanya matendo mema. Imani ya Abrahamu kwa Mungu kuhusu Isaka inamfanya Abrahamu kumheshimu Mungu kwenye wakati mgumu. Kwa kumheshimu Mungu imani yake ikakuwa.

kwa matendo imani yake ilifikia kusudio lake

Kwa kumwamini Mungu Abrahamu alitimiza kusudi la Mungu. "kwa kuwa Abrahamu alimtii Mungu alimwamini Mungu kabisa"

Maandiko yalitimia

"Hii ilitimiza maandiko"

Akahesabiwa kuwa ni mwenye haki

"Mungu aliiona imani yake kuwa imemfanya kuwa mwenye haki." Imani ya Abrahamu na haki vilimpa thamani.

mnaona

Yakobo tena anazungumza na hadhira yake kwa kutumia wingi toka kwenye umoja "wewe"

kwa matendo mtu huhesabiwa haki, na si kwa imani tu .

"Matendo na imani ndio yanayomfanya mtu kuwa na haki na sio imani tuu."

James 2:25

Hali kadhalika, ... haki kwa matendo

Yakobo alikuwa anasema kama ilivyokuwa kweli kwa Abrahamu ndivyo ilivyokuwa kweli kwa Rahabu. wote walihesabiwa haki kwa matendo.

hakuwa Rahabu yule kahaba alihesabiwa haki kwa matendo ... barabara nyingine

Yakobo alitumia swali kuwaelekeza watu. "hakuwa Rahabu yule kahaba alihesabiwa ... barabara nyingine."

Rahabu yule kahaba

Rahabu alikuwa mwanamke aliyezungumzwa katika agano la kale na Yakobo alitegema hadhira yake inafahamu.

haki kwa matendo

Yakobo anazungumzia matendo kama kitu cha kumiliki.

wajumbe

Watu wanaoleta habari njema toka sehemu nyingine.

kuwapeleka kwa barabara nyingine

"aliwasaidia kutoroka mjini"

Kwa kuwa kama vile mwili usipokuwa na roho umekufa, vivyo hivyo imani pasipo matendo imekufa.

Yakobo anazungumzia imani imani isiyo na matendo kama mwili uliokufa usio na roho.

James 3

Yakobo 03 Maelezo kwa jumla

Mifano muhimu katika sura hii

Mifano

Yakobo anawafundisha wasomaji wake kwamba waishi kumpendeza Mungu kwa kuwakumbusha kuhusu mambo wanayofahamu ya kawaida katika maisha ya kila siku. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

<< | >>

James 3:1

sio watu wengi

"siyo wengi wenu" Yakobo anatengeneza senyensi ya jumla.

Ndugu zangu

"wapendwa waumini wenzangu."

tutapokea hukumu kubwa sana

"Mungu atatuhukumu sisi kwa nguvu kwa sababu hatuna udhuru, wakati tufanyapo dhambi kwa sababu twajua na kufahamu Neno lake vizuri kuliko watu wengine."

Tutapokea

Yakobo anapanga makundi ya wale ambao hufundisha Maandiko kama yeye. Ingawa baadhi ya waumini ambao wangepokea barua hii, wangekuwa walimu wa Maandiko, wengi wasingeweza.

Kwa kuwa wote tunajikwaa.

Neno "wote" Yakobo amelitumia kumaanisha hadhira yake.

Kujikwaa

Dhambi imezungumzwa kama tendo la kujikwaa wakati wa kutembea. "kuanguka au kutenda dhambi"

Hawezi kujikwaa katika maneno yake.

"Hawezi kufanya dhambi kupitia maneno anayo zungumza."

Ni mtu mkamilifu.

"Amekomaa kiroho"

Kuongoza mwili wake wote.

Yakobo anazungumza juu ya moyo wake, hisia zake, na matendo yake. "kuongoza tabia yake" au "kuongoza matendo yake"

James 3:3

Ikiwa tunaweka rijamu kwenye midomo ya farasi.

Yakobo anazungumza kuhusu rijamu za farasi. Rijamu ni kipande kidogo cha chuma kinaachowekwa katika mdomo wa farasi ili kumuongoza kule anakoelekea.

Sasa ikiwa

"Kama" au "Endapo"

Farasi

"Farasi" ni mnyama mkubwa anayetumika kubeba vitu au watu. "endapo tunaweka rijamu katika vinywa vya farasi"

Tazama pia kwamba meli...huendeshwa kwa usukani mdogo sana.

"Meli" ni kama gari kubwa linaloelea juu ya maji. "Usukani"ni kipande kidogo cha mti au cha chuma kilicho nyuma ya meli kinachotumika kuiongoza meli kule inakoelekea. Neno "usukani" lingeweza kutafsiriwa kama "kifaa".

Maelezo ya jumla

Yakobo anajaribu kukuza mjadala juu ya vitu vidogo kutawala vitu vikubwa.

Zinasukumwa na kwa upepo mkali.

"Upepo mkali unazisukuma"

Zinaendeshwa kwa usukani mdogo sana popote nahodha atakapotaka kugeuka.

"Uwe na kifaa kidogo ambacho mtu anaweza kukitumia kuongozea meli mahali iendakako."

James 3:5

Vivyo hivyo.

Neno hili huashiria mlingano wa ulimi kwa rijamu za farasi na usukani wa meli katika mistari iliyotangulia.

Hujisifia mambo makuu sana

"mambo" ni ujumla wa vitu vyote ambavyo watu hawa wanajisifia.

Angalia

"fikiri kuhusu"

Jinsi msitu ulivyo mkubwa unawashwa na cheche moja!

"Ulimi mdogo wa moto unaweza kuwasha moto utakao unguza miti mingi!"

Ulimi pia ni moto.

Kama moto unavyo uunguza na kuteketeza vyote vinavyochomwa, ulimi, husimama badala ya mambo ambayo mtu huyatamka, yanaweza kuwaumiza watu vibaya. "Ulimi ni kama moto."

Ulimwengu wa uovu umewekwa katikati mwa viungo vya mwili wetu.

"Ni sehemu ndogo ya mwili wetu, lakini una uwezo wa kufanya dhambi katika aina zote za mambo."

Ambao hunajisi mwili wote.

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. "Inaweza kutufanya sisi tusimpendeze Mungu kabisa" au "Inaweza ikatufanya sisi tusikubalike kwa Mungu."

Na huweka katika moto njia ya uzima.

Msemo huu "njia ya uzima" una maana ya maisha yote ya mtu. "na unaweza kuharibu maisha yote ya mtu."

Na wenyewe unachomwa katika moto katika jehanamu.

Neno "wenyewe" limesimama badala ya ulimi. Pia, hapa neno "jehanamu" limesimama badala ya nguvu za uovu au nguvu za shetani. Hii ingeweza kutafsiriwa kama kishazi kazi: "kwa sababu shetani huutumia kwaajili ya uovu."

James 3:7

Kila aina ya .... na mwanadamu.

Usemi huu "kila aina" humaanisha "aina nyingi." hii inaweza kutafsriwa kama fungu la maneno yanayoonesha kutenda; "Watu wamejifunza kudhibiti aina nyingi za wanyama wa mwitu, ndege, vitambaavyo, na viumbe wa baharini."

Kitambaacho.

Huyu ni mnyama ambaye hutembea juu ya ardhi kwa kujikokota.

Kiumbe wa baharini

Huyu ni mnyama ambaye anaishi majini.

Lakini kuhusu ulimi hakuna hata mmoja miongoni mwa watu awezaye kuchunga ulimi.

Hapa "ulimi" humaanisha kile ambacho mtu hutamka. Maana kamili inaweza kutajwa kwa uwazi kama hivi: "hakuna mtu hata mmoja awezaye kudhibiti ulimi wake pasipo msaada wa Mungu."

Muovu asiyedhibitiwa

Ulimi umezungumziwa kama vile ni uovu usioweza kudhibitiwa. Yakobo anafananisha na tamaa za mtu kuongea mambo maovu.

Umejaa sumu ya kufisha

Yakobo anafananisha uwezo wa mtu kuongea mabaya kama vile nyoka au mmea wenye sumu. Sumu ni maneno yaumizayo ambayo yanaweza kusemwa kwa mtu.

James 3:9

Kwa ulimi tuna.

"Tunatumia ndimi zetu kusema maneno ambayo."

Tunawalaani watu.

Kumuomba Mungu awaumize wengine

Ambao wameumbwa katika sura ya Mungu.

"Ambaye Mungu amemfanya katika sura yake."

Kutoka kinywa kilekile inatoka baraka na laana

Maneno yaliyobeba baraka na laana yanatoka katika kinywa cha mtu.

Ndugu zangu.

"Wakristo wenzangu"

Mambo haya hayapaswi kuwa hivyo.

"Hili ni kosa."

James 3:11

Usemi unaounganisha.

Baada ya kuweka mkazo kwamba maneno ya waumini hayatakiwi kuwa ya baraka na laana, Yakobo anatoa mifano ya kufundisha wasomaji wake kuwa watu wanamheshimu Mungu kwa kuishi katika njia sahihi.

Je, chemchemi moja hutoa maji matamu na machungu?

Yakobo anatumia swali lisilodai jibu kuwafundisha wasomaji kuhusu sanjari ya mpangilio wa maumbile. "Chemchemi moja haitoi maji matamu na machungu."

Ndugu.

"Waumini wezangu"

Je,mti wa mtini huzaa mizeituni, au mzabibu huzaa matunda ya mtini?

Yakobo anatumia neno la picha ya umbo kuwafundisha wasomaji kuhusu sanjari ya mpangilio wamaumbile. "Mtini hauwezi kuzaa mzeituni, wala mzabibu hauzai matunda ya mtini"

James 3:13

Nani miongoni mwenu ana hekima na ufahamu? Haya mtu huyo.

Yakobo anatumia swali hili kufundisha wasikilizaji wake kuhusu tabia ya unyofu. Maneno " hekima" na "ufahamu" ki-msingi yana maana ileile. "Mtu ambaye ana fikiri kuwa ana hekima sharti"

Onesha maisha mema.

"Onesha tabia njema" au "Ioneshe"

Kwa matendo yake katika unyenyekevu ambao unatoka katika hekima.

"Pamoja na matendo yake mema na unyenyekevu ambao hutokana na kuwa na hekima ya kweli."

Kuwa na wivu mkali na nia ya ubinafsi katika mioyo yenu.

Neno "moyo" hapa lina maana ya jaziba au fikra. "Hutapenda kushiriki jambo na wengine na daima unajiweka mwenyewe katika nafasi ya kwanza."

Usijiinue na kuwa kinyume na ukweli.

"Usiseme uongo na kujifanya kama una hekima."

James 3:15

Hii siyo

"Hii" inarejea katika wivu wa kijinga na nia za ubinafsi kama zilivyoelezwa katika mistari iliyipita.

Hekima ishukayo chini kutoka juu

Ubora wa hekima inayozungumziwa ni kana kwamba ni ile ambayo Mungu aliituma chini toka mbingune

Niya kidunia.

Neno "niya kidunia" humaanisha thamani na tabia za watu ambao hawamheshimu Mungu. "Kutomheshimu Mungu."

Ni ya kishetani.

"Bali ni kutoka kwa mapepo."

Kwa sababu mahali palipo na wivu na nia ya ubinafsi.

"Kwa sababu popote palipo na watu ambao hujihudumia wao binafsi bila kujali wengine."

Kuna ghasia.

"Kuna vurugu" au "kuna mtafaruku."

Kila tabia ya uovu.

"Kila aina ya tabia ya dhambi" au "kila aina ya tendo la uovu."

Kwanza ni safi.

"Kwanza ni takatifu."

Kisha yenye amani na upendo.

Inayopenda- "kisha ni yenye amani."

Yenye wema

Yenye moyo- "wema" au "yenye kujali."

Na tunda jema.

Tunda hili jema linalinganishwa na matendo mema. "matendo mema"

Kamilifu

"Yenye kuaminika" au "yenye ukweli."

Na tunda la haki limepandwa katika amani kwa wote watendao mambo ya amani.

Hii inalinganisha amani na haki katika maisha yetu kama kupanda na kuvuna mazao. "wale ambao huishi katika amani wanafafanya ambacho Mungu husema ni haki."

Si ya kiroho.

"Si ya kutoka kwa Roho Mtakatifu" au "si ya kiroho."

Juu

Hapa "juu" inamaanisha Mungu

James 4

Yakobo 04 Maelezo kwa jumla

Dhana muhimu katika sura hii

Uzinzi

Wandishi katika Bibilia huzungumzia mara nyingi uzinzi kama mfano kwa watu wanaosema wanampenda Mungu lakini wanatenda mambo Mungu huchukia. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#godly)

Sheria

Kuna uwezekano Yakobo analitumia neno hili katika Yakobo 4:11 kumaanisha "sheria ya kifalme" (Yakobo 2:8) na siyo sheria ya Musa(Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lawofmoses)

Mifano muhimu ya usemi katika sura hii

Maswali ya kana

Yakobo anauliza maswali mengi kwa sababu anataka wasomaji wake wafikirie jinsi wanavyoishi. Anataka kuwarekebisha na kuwafudisha. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-rquestion)

Maswala mengine ya utata katika tafsiri ya sura hii

Nyenyekevu

Kuna uwezekano neno hili hutumika kumaanisha watu wasiyo na majivuno. Yakobo analitumia neno hili kuashiria watu wasiyokuwa na majivuno na wanaoeza kumtumainia Yesu na kumtii.

<< | >>

James 4:1

Sentensi unganishi

Yakobo anawakemea waamini waliokosa unyenyekevu. Anawaonya kuwa makini na namna wanavyozungumza na watu wengine.

Maelezo ya jumla

Maneno "ninyi, wewe" imetumika kama wingi kuwaelezea waamini walioandikiwa na Yakobo.

ugovi unatoka wapi ... migogoro

Maneno "ugonvi, migogor" yanamaanisha kitu kimoja. Yakobo anayatumia kusisitiza kuwa nazungumzia juu ya mvutano kati ya watu.

ugonvi na migogoro

Ni tabia zinazotokea katika jamii

Haviinuki kutoka katika tamaa zenu mbaya zinazoleta vita

Yakobo anatumia swali kukemea hadhira yake. "ni kwa sababu mna tamaa mbaya" "kwa sababu mnatamani vitu vibaya"

Haviinuki kutoka katika tamaa zenu mbaya zinazoleta vita ndani ya washirika wenu?

Yakobo anazungumzia tamaa kama adui anayeleta vita kati ya waamini. kwa hali halisi ni watu ndio wenye tamaa hizi na kugombana wenyewe kwa wenyewe. "mnatamani maovu na mwishoni nmaumizana wenyewe kwa wenyewe"

Ndani ya washirika wenu

Yaweza kuwa na maana kuwa 1) kuna ugonvi kati ya waamini au 2) vita ambayo ni ugonvi upo ndani ya kila mwamini.

Mnauwa na mnafukuzia kile msichoweza kuwa nacho.

"mnauwa" inaelezea ni kwa kiasi gani watu wanaweza kufanya lolote baya ili wawezea kupata wanachokitaka. "Mnafanya uovu wa kila namna ili mpate msichoweza kukipata"

Mnapigana na kugombana

"kupigana na kugombana" zinamaanisha kitu kimoja. Yakobo anatumia kusisitiza namna ambavyo watu wanagombana wenyewe kwa wenyewe.

Mnaomba vibaya

Yaweza kuwa na maana kuwa 1) mnaomba mkiwa na nia mbaya au 2) mnaomba vitu ambavyo hampaswi kuomba au mnaomba vitu vibaya.

James 4:4

Enyi wazinzi

Yakobo anazungumza na waamini akiwafananisha na mke aliyelala na mwanaume mwingine ambaye sio mume wake. "ninyi sio waaminifu kwa Mungu"

Hamjui kwamba ... Mungu?

Yakobo alitumia hili swali kuifundisha hadhira yake. "Mnajua ... Mungu"

urafiki na ulimwengu

Maneno haya yanaelezea uhusiano uliopo kwenye mifumo ya duniani na tabia zake.

urafiki na ulimwengu

Hapa mfumo wa ulimwenguni unaelezewa kama vile ni mtu ambaye watu wengine wanaweza kuwa na urafiki naye.

urafiki na ulimwengu ni uadui dhidi ya Mungu

Kuwa rafiki na ulimwengu inamaanisha kuwa adui wa Mungu. "urafiki na dunia" inamaanisha watu ambao ni marafiki wa dunia na "uadui dhidi ya Mungu" inamaanisha watu ambao wanampinga Mungu. "Marafiki wa ulimwengu ni maadui wa Mungu"

Au mnadhani maandiko hayana maana

Yakobo anatumia swali kueleza kuwa "Kuna maana katika maandiko"

Roho aliyoweka ndani yetu

Tafisi nyingine zinaelezea "roho" kama Roho Mtakatifu. Na tafsiri zingine zinamaanisha roho ya binadamu ambayo kila mtu ameumbwa nayo. Tunapendekeza kuwa utumie maana nyingine ambayo ipo katika tafsiri zinazotumika na wasomaji wako.

James 4:6

Lakini Mungu hutoa neema zaidi

"Japokuwa nafsi zetu hutamani tusivyoweza kuvipata, Mungu atatupa zaidi neema, tukijinyenyekeza wenyewe"

Hutoa neema zaidi

Neema imezungumzwa kama kitu kinachoweza kutolewa.

Kiburi

"mtu mwenye kiburi"

nyenyekea

"mtu mnyenyekevu"

Hivyo

"Kwa sababu hii"

Jitoeni kwa Mungu

"mtii Mungu"

Mpingeni ibilisi

"mpingine ibilisi" au "Msifanye mambo ambayo ibilisi anawaambia mfanye"

atakimbia

"atakimbia mbali"

ninyi

Hii inamaanisha hadhira ya Yakobo.

James 4:8

Taarifa ya jumla.

Neno "ninyi" linamaanisha waamini waliotawanyika ambao Yakobo anawaandikia.

Sogeeni karibu na Mungu, na yeye atakaribia karibu nanyi

Hapa anamaanisha kuwa wakweli na wazi kwa Mungu.

Safisheni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na takaseni mioyo yenu, enyi wenye nia mbili.

Hizi ni sentensi mbili zinazoendana.

Safisheni mikono yenu

Hii ni amri kwa watu kufanya mambo ya haki na sio maovu. "Ishini namna ambavyo inampendeza Mungu"

Takaseni mioyo yenu

"mioyo" inamaanisha mawazo ya mtu na hisia zake" Mheshimu Mungu kwa mawazo yako"

nia mbili

"Nia mbili" linamaanisha mtu ambaye hawezi kufanya maamuzi juu ya jambo fulani. "Mtu ambaye hawezi kuamua amtii Mungu au la"

Huzunika, omboleza, na Lia

Maneno haya matatu yana maana moja. Yakobo anayatumia kwa pamoja kuonesha kuwa watu watahuzunika sana kwa kutokumtii Mungu" Yakobo anasema haya kama amri.

Geuzeni kicheko chenu kuwa huzuni na furaha yenu kuwa maombolezo

Hapa kicheko kimezungumzwa kuwa kitageizwa kuwa huzuni na furaha kuwa maombolezo. "Acheni kucheka na mtubu kwa Mungu"

Nyeyekeeni wenyewe mbele za Bwana

"Jinyenyekezeni mbele za Mungu"

Atawainua juu

Yakobo anazungumza namna ambavyo Mungu anamuheshimu mtu mnyenyekevu na kumnyanyua toka chini. "atakuheshimu wewe"

James 4:11

Maelezo ya jumla

Maneno "wewe" au "ninyi" yametumika kuwaelezea waamini walioandikiwa na Yakobo.

Kunena kinyume

"kusema vibaya kuhusu" au "kupinga"

Ndugu

Yakobo anawazungumzia waamini kama ndugu waliozaliwa pamoja. "waamini wenzangu"

bali mnaihukumu

"bali mnafanya kama mtu anayetoa sheria"

Ni mmoja tu ambaye ni mtoa sheria na hakimu

Hapa anamaanisha Mungu. "Mungu ndiye atoaye sheria na ahukumuye"

Wewe ni nani ambaye unamhukumu jirani yako?

Yakobo anatumia swali hili kuikemea hadhira yake. "Ninyi ni binadamu na hamuwezi kuwahukumu binadamu wengine"

James 4:13

kukaa huko mwaka

Yakobo anazungumzia kutumia mda kama pesa. "kaeni huko mwaka mzima"

Ni nani ajuaye nini kitatokea kesho

Yakobo anatumia swali hili kuisahihisha hadhira yake. "Hakuna ajuaye kitakachotokea kesho"

maisha yenu ni nini hasa?

Yakobo alitumia swali hili kufundisha waamini kuwa maisha ya kimwili sio ya muhimu sana. "fikirini juu ya maisha yenu ya kimwili"

Kwa kuwa mnafanana kama ukungu unaotokea kwa muda mfupi na kisha hupotea.

Yakobo anawafananisha watu na ukungu ambao hutokea na kupotea kwa haraka. "mnaishi kwa muda mfupi na kufa"

James 4:15

Badala yake mngesema

Badala yake, mtazamo wenu uwe?"

sisi tutaishi

Neno "sisi" halimaanishi Yakobo au hadhira yake lakini ni mfano wa namna ambavyo hadhira ya Yakobo inatakiwa iishi.

tutafanya hiki au kile.

"kufanya kile ambacho tumepanga kufanya"

kwake yeye ajuaye kutenda mema lakini hayatendi, kwake huyo ni dhambi.

Yeyote anayeshindwa kufanya jambo ambalo anapaswa kufanya anatenda dhambi.

James 5

Yakobo 05 Maelezo kwa jumla

Dhana muhimu katika sura hii

Milele

Sura hii inatofautisha vitu vya dunia hii ambavyo havidumu na kuishi kwa ajili ya vitu vitakavyodumu milele. Ni vyema pia kuishi na matarajio kwamba Yesu atarudi karibuni. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#eternity)

Viapo

Wasomi wanatofautiana iwapo fungu hili linafundisha kwamba viapo vyote ni vibaya. Wasomi wengi wanakubaliana kwamba viapo vingine vinakubalika na badala yake Yakobo anawafundisha Wakristo kuwa na maadili.

Maswala mengine ya utata katika tafsiri ya sura hii

Eliya

Hadithi hii itakuwa ngumu kuelewa iwapo vitabu vya 1 Wafalme na 2 Wafalme na 1 Mambo ya Nyakati na 2 Mambo ya Nyakati havijatafsiriwa.

"Okoa roho yake kutoka kwa kifo"

Huenda hii inafundisha kwamba mtu anayeacha maisha yake ya dhambi hataadhibiwa na kifo cha mwili kama athari ya dhambi yake. Kwa upande mwingine, wasomi wamoja wanaamini kwamba hili fungu linafundisha kuhusu wokovu wa milele. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#death and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#save)

__<< | __

James 5:1

Sentensi unganishi

Yakobo anawaonya matajiri juu ya starehe na utajiri.

enyi mlio matajiri

Yaweza kuwa na maana ya 1) Yakobo anawapa onyo kali wale wanaoamini kwenye utajiri au 2) Yakobo anazungumza kuhusu watu wasioamini ambao ni matajiri. "enyi mlio matajiri na mnaosema mnamcha Mungu"

kwa sababu ya taabu inayokuja juu yenu

Yakobo anaelezea kuwa watu hao watateseka sana baadae na taabu yao inakuja. "kwa kuwa mtateseka sana baadae"

Utajiri wenu umeharibiwa na mavazi yenu yametafunwa na wadudu waharibifu. Dhahabu zenu na fedha zenu zimekosa thamani

imetafunwa. Dhahabu zenu na fedha zimekosa thamani. Yakobo anazungumza juu ya matukio haya kama vile yameshatokea. Yakobo anazungumzia utajiri wa duniani haudumu na hauna uzima wa milele. "Utajiri wenu umeharibiwa, nguo zenu zimetafuwa na dhahabu zenu na fedha zimekosa thamani"

utajiri ... nguo ... dhahabu

Hivi vitu vimetajwa kama mifano ya vitu vya thamani kwa mwanadamu.

uharibifu wake utashuhudia dhidi yenu

"uharibifu" ni neno linaloelezea namna ambavyo chuma yaweza haribika. Yakobo anazungumzia kuhusu uharibifu kwa kuwa umesababishwa na watu waovu na matendo yao. "Na Mungu akiwahukumu kuharibiwa kwa mali zenu kutakuwa kama mtu anayewahukumu mahakamani"

Itaangamiza ... kama moto

Uharibifu unazungumzwa kama vile moto ambao utakuja kuwaangamiza watu.

Miili yenu

"mwili" inamaanisha mwili mzima.

Moto

Moto inatumika kuwakumbusha watu kwamba mara nyingi inamaanisha hukumu ya Mungu itakayokuja juu ya waovu.

Katika siku ya mwisho.

Hii inaelezea wakati muafaka wa Mungu kuja kuhukumu ulimwengu. Waovu wanadhani wanahifadhi utajiri kwa ajili ya baadae lakini wanachokifanya wanahifadhi hukumu. "wakati ambao Mungu anataka kuwahukumu"

James 5:4

Sentensi unganishi

Yakobo anaendelea kuwaonya matajiri juu ya starehe na utajiri.

malipo ya watendakazi-wale ambao hamjawalipa kwa kuvuna katika mashamba yenu- wanalia

Pesa ambayo ilitakiwa ilipwe imeelezewa hapa kama mtu anayelalamika juu ya dhuluma aliyofanyiwa. "kwa kuwa hamwalipi mliowaajiri kufanya kazi kwenye mashamba yenu mnafanya makosa"

kilio cha wale waliovuna mazao yenu kimeyafikia masikio ya Bwana wa Majeshi.

Kilio cha wanaovuna kimesikika mbinguni. "Bwana wa majeshi amesikia kilio cha wavunaji"

kwenye masikio ya Bwana wa Majeshi

Mungu anazungumziwa kuwa ana masikio kama mwanadamu. "Bwana wa majeshi amesikia"

Mmejinenepesha mioyo yenu kwa siku ya machinjo

Hapa watu wanaelezewa kama wanyama, wanaolishwa vizuri ili wanenepe na kuchinjwa kwa ajili ya karamu. Japokuwa hamna atakayesherehekea siku ya hukumu. "Tamaa zeni zinawaandaa kwa hukumu ya milele"

mioyo yenu

"Mioyo" imezungumziwa kama kituo cha tamaa za mwanadamu. Neno hili linasimama kumuelezea mtu kwa ujumla.

Mmemhukumu ... mwenye haki

"Mmehukumu" inaweza isiwe na maana ya kisheria ya kupitisha hukumu ya kifo. Bali inawazungumzia watu waovu na wenye nguvu wanaoamua kuwanyanyasa masikini mpaka wanakufa.

mwenye haki

"Mtu anayefanya mambo yanayofaa" Hii sentensi inaelezea watu wenye haki kwa ujumla na sio mtu mmoja.

asiyeweza kuwapinga

"Asiye kinyume na ninyi"

James 5:7

Sentensi unganishi

Yakobo anabadilisha mada toka kwenye kuwakemea matajiri na kuwapa mawaidha waamini.

Maelezo ya jumla

Kwa kufunga Yakobo anawakumbusha waamini kuhusu ujio wa Bwana na kuwapa mafundisho mafupi namna ya kuishi kwa ajili ya Mungu.

Kwa hiyo vumilieni

"Kwa ajili ya hili kuweni na subira na uvumilivu"

mpaka ujio wa Bwana

Sentensi hii inaelezea ujio wa Yesu, atakapoanzisha ufalme wake duniani na kuhukumu watu wote. "Mpaka Kristo atakapokuja"

Mkulima

Katika mazungumzo haya Yakobo anatumia mkulima na mwamini kuelezea namna ya kuwa mvumilivu.

Kazeni mioyo yenu

Yakobo anawataka waamini wawe na mioyo thabiti na kuwa na msimamo. "Kuweni na msimamo" au "Ifanyeni imara mioyo yenu"

kuja kwake Bwana ni karibu.

"Bwana atarudi mapema"

James 5:9

Nsinung'unikiane, ndugu ... ninyi

Yakobo anawaandikia waamini wa Kiyahudi waliotawanyika.

ninyi kwa ninyi,

"kila mmoja na mwenzake"

Hamtahukumiwa

Hii yaweza kuwa "Kristo hatawahukumu ninyi"

hakimu anasimama mlangoni

Yakobo anamfananisha Yesu, kama hakimu kwa mwanadamu na kuelezea ni kuwa bado mda mfupi sana Yesu atarudi kuhukumu ulimwengu"

mateso na uvumilivu wa manabii

"ni kwa namna gani manabii walivumilia mateso na hukumu"

walionena katika jina la Bwana

"Waliongea kwa jina la Bwana kwa watu"

Tazama

"Tazama" inasisitiza "sikiliza kwa makini" au "kumbuka"

wale wanaovumilia

"Wale watakaoendelea kumtii Mungu hata katika hali ngumu"

James 5:12

Zaidi ya yote

"Hii ni muhimu" au "Hasa"

ndugu zangu

"waamini wenzangu"

msiape

"kuapa" ni kusema kuwa utafanya jambo au jambo fulani ni kweli na kuwa na wajibu kwa mamlaka za juu. "Msiape"

aidha kwa mbingu ama kwa nchi

Maneno "mbingu" na "nchi" linamaanisha mamlaka ya kiroho na kibinadamu zilizopo mbinguni na duniani.

"ndiyo" yenu na imaanishe "ndiyo" na "hapana" yenu na imaanishe "hapana

Fanya ulichosema utafanya bila kuapa"

msije kuangukia chini ya hukumu

Kuhukumiwa inazungumzwa kwa mtu aliyeanguka na kulemewa na kitu kizito. "Hivyo Mungu hatawahukumu"

James 5:13

Kuna yeyote miongoni mwenu ana mateso? Lazima aombe

"Kama kuna mtu yeyote anapata mateso yampasa kuomba"

Je, mtu yeyote ni mwenye kuchangamka? Na aimbe sifa

"Mtu yeyote akiwa na furaha, yampasa aimbe nyimbo za kusifu"

Je, kuna yeyote miongoni mwenu aliye mgonjwa? Na aite

"Mtu yeyote akiwa mgonjwa na aite watu"

maombi ya imani yatamponya mgonjwa, na Bwana atamwinua

Mwamini akimuombea mgonjwa, Mungu atasikia maombi yake na kumponya mtu huyo. "Mungu atasikia maombi ya mwamini aombapo kwa imbani na kumponya mgonjwa.

James 5:16

Maelezo ya Jumla

Kwa kuwa haw walikuwa waamini wa kiyahudi, Yakobo anawakumbusha watu kuomba kwa kukumbuka moja wa manabii na namna walivyoomba.

Kwa hiyo ungameni dhambi zenu

Hii ni kukubali makosa yako kwa waamini wengine ili uweze kusamehewa.

ninyi kwa ninyi,

"kila mmoja na mwenzake"

ili muweze kuponywa

"Ili Mungu awaponye"

Maombi ya mwenye haki huzaa matokeo makubwa

Maombi ni kitu chenye nguvu sana. "Mtu anayemcha Mungu akiomba, Mungu anafanya mambo makuu"

Juhudi

"shauku"

Tatu ... sita

"3 ... 6"

mbingu zilimwaga mvua

Mbingu inamaanisha mawingu ambayo inaelezwa kama chanzo cha mvua. "Mvua ilishuka toka mawinguni"

nchi ikatoa mavuno.

Hapa nchi inaelezwa kama chanzo cha mavuno

Matunda

"Matunda" inamaanisha mazao ya mkulima

James 5:19

Ndugu zangu

"Waamini wenzangu"

kama yeyote miongoni mwenu anapotoka kutoka kwenye ukweli, lakini mtu mwingine akamrejesha

Mwamini ambaye anaacha kumwamini Mungu na kumtii yeye anafananishwa na kondoo aliyeondoka kwenye kundi. Mtu anayemrejesha ili amwamini Mungu tena anafananishwa na mchungaji anayetafuta kondoo aliyepotea. "Mtu yeyote akiacha kumtii Mungu na mwingine akamsaidia kuanza kumtii Mungu tena"

yeyote amwongozaye mwenye dhambi kuondoka katika njia yake ya ukosaji... atafunika wingi wa dhambi.

Yakobo anamaanisha kuwa Mungu atatumia matendo ya huyu mtu ya kumrejesha aliyekosa ili atubu na kuokolewa. Lakini Yakobo anaongea kama vile huyu mtu mwingine ndo ameokoa nafsi ya mwenye dhambi toka kwenye kifo.

ataponya nafsi yake kutoka katika mauti na atafunika wingi wa dhambi.

Hapa "kifo" inamaanisha kufa kiroho, kutengana na Mungu. "Atamuokoa na kifo cha kiroho na Mungu atamsamehe mkosaji dhambi zake zote"

atafunika wingi wa dhambi.

Yawza kumaanisha kuwa 1) Mtu atakayemrejesha ndugu aliyetenda uovu, dhambi zake zitasamehewa. au 2) Ndugu aliyetenda uovu akirudi kwa Bwana , dhambi zake zitasamehewa. Dhambi inazungumzwa kama jambo ambalo Mungu atawasamehe watu wake.

Utangulizi wa 1 Petero

Sehemu ya 1 Utangulizi wa jumla

Muhtasari wa 1 Petero

  1. Utangulizi (1:1-2)
  2. Shukrani kwa ukombozi wa Mungu kwa waumini (1:3-2:10)
  3. Maisha ya Kikristo (2:11-4:11)
  4. Utiaji wa moyo kuvumila wakati wa mateso (4:12-5:11)
  5. Kufunga (5:12-14)

Nani aliandika kitabu cha 1 Petero?

Kitabu cha 1 Petero kilandikwa na mtume Petero. Aliwaandikia Wakristo Wayahudi waliotawanyika katika Asia Ndogo

kitabu cha 1Petero kinahusu nini?

Petero alibainisha kwamba aliandika barua hii kwa ajili ya "kukutia moyo na kushahidia kwamba hii ndiyo neema ya kweli ya Mungu" (5:12). Aliwahimiza Wakristo kuendelea kumtii Mungu hata wakiwa kwenye mateso. Aliwaambia wafanye hivi kwa sababu Yesu angerudi karibuni.Petero pia alitoa maelezo kuhusu kuheshimu watu walio na mamlaka.

Kichwa cha kitabu hiki kitafsiriwe namna gani?

Watafsiri wanweza kuamua kukiita kitabo hiki na jina lake la kiasili, 1 Petero", ama "Petero wa Kwanza" ama wanaweza kuchagua kichwa kinachoeleweka zaidi kama "Barua ya kwanza kutoka kwa Petero" ama "Barua ya kwanza alioandika Petero."(Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-names)

Sehemu ya 2: Dhana muhimu za kidini na Kitamaduni

Wakristo walitendewa kivipi Roma?

Kuna uwezekano Petero alikuwa Roma akiandika barua hii. Aliupa mji wa Roma jina la mfano ya "Babeli" (5:13). Inaonekana wakati Petero anaandika barua hii, Warumi walikuwa wanawatesa vibaya sana Wakristo.

Sehemu ya 3: Maswala muhimu ya tafsiri

Umoja na wingi wa "wewe" na "nyinyi"

Katika kitabu hiki "Mimi" inaashiria Petero isipokuwa kwa sehemu mbili: 1 Petero:1:6 na 1 Petero 2:6. Neno "nyinyi" limetumika kwa wingi kuashiria hadhira ya Petero. (Tazama: : https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-you)

Ni maswala gani muhimu katika maandishi ya kitabu cha 1 Petero?

Iwapo tafsiri ya Bibilia ipo katika eneo kwa jumla, watafsiri wanafaa kuzingatia kutumia masomo yanayopatikana katika matoleo hayo. Kama sivyo watafsiri wanashauriwa kufuata masomo ya kisasa.

(See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/jit.html#translate-textvariants)

1 Peter 1

1 Petero 01 Maelezo kwa jumla

Muundo na Mpangilio

Watafsiri wengine wametenga mistari ya ushairi mbele zaidi kuelekea kulia kuliko maandishi mengine ili yasomeke kwa urahisi. ULB hufanya hivi na ushairi ambao umenukuliwa kutoka Agano la kale katika 1:24-25.

Dhana maalum katika sura hii

Kile Mungu anafunua

Yesu atakaporudi tena, kila mtu ataona jinsi watu wa Mungu walikuwa wawe na imani kwa Yesu. Halafu watu wa Mungu wataona jinsi Mungu amekuwa wa neema kwao na watu wote watamsifu Mungu na watu wake.

Utakatifu

Mungu anataka watu wake wawe watakatifu kwa sababu Mungu ni Mtakatifu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#holy)

Milele

Petero anawaambia watu kuishi kwa ajili ya vitu vya kudumu milele na kuacha kuishi kwa ajili ya vitu vya dunia hii ambavyo vitaisha. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#eternity)

Maswala mengine ya utata katika sura hii

Ukweli kinza

Ukweli kinza ni kauli ya ukweli ambayo inaonekana kuelezea kitu kisichowezekana. Petero anaandika kwamba wasomaji wake wanafurahi na kuhuzunika kwa wakati mmoja (1 Petero 1:6). Anaweza kusema hivi kwa sababu wanahuzuni kwa sababu wanateseka lakini wanafurahi kwa sababu wanafahamu kwamba Mungu atawaokoa nyakati za mwisho" (1 Peter 1:5)

| >>

1 Peter 1:1

Petro, mtume wa Yesu Kristo

Petro anajitambulisha mwenyewe. "Mimi, Petro, mjumbe wa Yesu Kristo ninawaandikia (wingi

Ponto

Hii ni siku ya sasa kaskazini mwa Uturuki.

Galatia

Hii ni siku ya sasa ya kati Uturuki.

Kapadokia

Hii ni siku ya sasa mashariki ya kati Uturuki.

Asia

Hii ni siku ya sasa magharibi ya kati Uturuki.

Bithinia

Hii ni siku ya sasa kaskazini magharibi Uturuki.

foreknowledge

Maana iwezekuwa ni kwamba 1) Mungu anajua tukio kabla ya kutokea au 2) Mungu 'aliamua awali' (UDB).

kuinyunyiza damu yake

Hii ina maana ya damu ya Yesu kama dhabihu na wakati Musa aliponyunyiza damu kwenye taifa la Israeli.

Neema iwe kwenu

Maneno "Neema iwe kwenu" ni salamu za kawaida za watu anaowaandikia. Katika lugha zingine ni kawaida kuweka salamu zako za kawaida hapa. Neno "wewe" na lako" linamaanisha waumini wanaoishi katika maeneo yaliyotajwa hapa juu.

1 Peter 1:3

Bwana wetu Yesu Kristo

Maneno "yetu" na "sisi" yanataja msemaji (Petro) na waumini waliotajwa

Alitupa kuzaliwa upya

Mwandishi anazungumzia kuhusu kuzaliwa kwa kiroho tuliyopewa tu na Yesu. AT "ametufanya tuishi tena."

kwa ujasiri wa urithi

"tunajua kwamba atatufanyia yale aliyoahidi" (UDB)

zimehifadhiwa

"kuokolewa kwa ajili yetu" au "kuhifadhiwa kwa ajili kwetu" (UDB)

haitakuwa na madhara

"hawezi kuumiza na dhambi au 'dhambi haiwezi kuumiza"

katika nyakati za mwisho

"wakati Kristo anarudi duniani"

1 Peter 1:6

Unafuraha katika hili

Neno hili linamaanisha baraka zote za "hufurahi kwa kile Mungu amefanya"

sasa ni muhimu kwako kujisikia huzuni

"sasa ni sawa na sahihi kwamba unajisikia huzuni"

hiyo ni ya thamani zaidi kuliko dhahabu

"Mungu hufurahia imani yako zaidi kuliko yeye anayegundua dhahabu"

ipi huangamia katika moto ambayo inachunguza imani yako

"ingawa dhahabu hujaribiwa na moto, haiwezi kudumu milele"

katika ufunuo wa Yesu Kristo

"wakati Yesu Kristo anarudi"

1 Peter 1:8

Hukumwona

"Hukumwona kwa macho yako mwenyewe" au "hujamwona kimwili." Matukio yote ya "wewe" rejelea kwa waumini katika [1 pe:01:01]

1 Peter 1:11

Walitaka kujua

"Walijaribu kujua" au "Waliuliza kuhusu"

Wao

Neno "wao" linamaanisha manabii.

Ilifunuliwa kwa manabii

"Mungu alifunua unabii wa Kristo kwa manabii"

walikuwa wakitumikia mambo haya, si kwao wenyewe, bali kwa ajili yenu

Kwa lugha zingine ni kawaida zaidi kuweka chanya kabla ya hasi. AT "walikuwa wakutumikia mambo haya kwa ajili yenu, sio wenyewe."

kutumikia mambo haya

Walikuwa wanatafuta kuelewa unabii kuhusu Kristo.

1 Peter 1:13

Panda viuno vya akili yako

Wakati wa kuvaa vazi, mtu angeweza kufunga vazi hilo kwa mkanda wake kujiandaa kwa ajili ya kazi. AT "huandaa mawazo yako kwa shughuli."

Kuwa na busara katika kufikiri kwako

AT "Kudhibiti mawazo yako" au "Jihadharini na nini unafikiri."

1 Peter 1:15

Mmoja

Mungu

Kwa maana imeandikwa

"Kwa maana kama Musa alivyoandika zamani."

bila upendeleo

"haki"

kutumia muda wa safari yako kwa heshima

"Ishi kwa kumheshimu Mungu wakati unapokaa Duniani"

1 Peter 1:18

umekombolewa kutoka

"Mungu amekukomboa kutoka" au "Mungu amekuokoa kutoka.?

kama wa kondoo

Yesu alikufa kama dhabihu ili Mungu atasamehe dhambi za watu.

bila ya ukamilifu na bila doa

Petro anaonyesha wazo sawa katika njia mbili tofauti za kusisitiza usafi wa Kristo. AT "bila kutokamilika."

1 Peter 1:20

Kristo alichaguliwa

"Mungu amemchagua Kristo."

kabla ya msingi wa ulimwengu

"Kabla ya kuumbwa ulimwengu"

amefunuliwa kwako

"Mungu amemfanya ajulikane kwako."

1 Peter 1:22

upendo wa ndugu

Huu ni upendo wa kibinadamu kati ya marafiki au jamaa.

Pendaneni ninyi kwa ninyi kwa dhati kutoka moyoni

Pendaneni nyinyi kwa nyinyi kwa undani na kwa dhati

Umezaliwa tena ... kutoka mbegu isiyoharibika

Petro ni sawa na uzao wao wa kiroho kwa mbegu ambayo haitakufa kamwe. Wao wataishi kwa milele.

kuharibika

"sio kuharibika" au "kudumu"

kupitia maisha ...neno la Mungu

Neno lililo hai la Mungu linamaanisha neno la Mungu uwezo wa kubadili maisha ya watu wakati wote kama kama mtu halisi anayehubiri na kufundisha watu kuhusu Mungu.

1 Peter 1:24

nyama zote ni kama nyasi

"watu wote wataangamia kama majani huharibika." (UDB)

Utukufu wake wote ni kama maua ya nyasi

"na ukuu wote ambao watu wanao hautaendelea milele." (UDB)

ujumbe ambao uliotangazwa

"ujumbe ambao tuliutangaza."

1 Peter 2

1 Petero 02 Maelezo kwa jumla

Muundo na mpangilio

Watafsiri wengine wametenga mistari ya ushairi mbele zaidi kuelekea kulia kuliko maandishi mengine ili yasomeke kwa urahisi. ULB hufanya hivi na ushairi ambao umenukuliwa kutoka Agano la kale katika 2:6, 7, 8 na 22.

Dhana muhimu katika sura hii

Mawe

Bibilia inatumia jengo lililojengwa kwa mawe makubwa kama mfano wa kanisa. Yesu ni jiwe kuu la pembeni, jiwe la muhimu. Mitume na manabii ndio msingi, sehemu ya jengo hili ambamo mawe mengine yanasimamia. Katika sura hii Wakristo ni mawe ambayo yanatengeneza kuta za jengo. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#cornerstone and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#foundation)

Mifano muhimu za usemi katika sura hii

Maziwa na watoto

Wakati Petero anawaambia wasomaji wake kwamba "watamani maziwa halisi ya kiroho", anatumia mfano ya mtoto mchanga ambaye hawezi kula chakula kigumu. Anataka kuwaelezea wasomaji wake kwamba wanaweza tu kuelewa vitu rahisi kuhusu maisha ya kumfurahisha Mungu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

<< | >>

1 Peter 2:1

Kw ahiyo, weka pembeni

"Basi kuacha kufanya"

Kama watoto wachanga, tamaa kwa maziwa safi ya kiroho

Kama watoto wazaliwa wapya wanatamani maziwa ya mama zao, hivyo waumini wapya waliozaliwa kiroho wanapaswa kutamani neno la Mungu. Neno la Mungu pia linajulikana kama maziwa safi ya kiroho.

Kama watoto wachanga

Wakati mmoja akizaliwa kiroho, wanahitaji kusoma neno la Mungu kuishi na kukua kama mtoto mpya aliyezaliwa anahitaji kunywa maziwa ili kuishi na kukua

kwa muda mrefu

"hamu sana" au "tamani"

unaweza kukua katika wokovu

"unaweza kukua kiroho." Neno "wewe" linamaanisha waumini waliotajwa katika sura ya 1.

ikiwa umeonja kuwa Bwana ni mwema

"kwa sababu umeona kwamba Bwana hutendea kwa huruma kwako" (UDB)

1 Peter 2:4

Njoo kwa yeye aliye jiwe la uzima

Petro anafananisha Yesu na jiwe muhimu zaidi katika msingi wa jengo.

ambayo imekataliwa na watu

"kwamba watu wengi walikataliwa."

lakini hiyo imechaguliwa na Mungu

"lakini Mungu amechagua."

Wewe pia ni kama ... nyumba ya kiroho

Kama vile mawe hutumiwa kujenga nyumba, Mungu anatuletea pamoja ili kujenga nyumba yake ya kiroho au familia.

ambazo zinajengwa kuwa nyumba ya kiroho

kwamba Mungu anajenga ndani ya nyumba ya kiroho.

1 Peter 2:6

Andiko linasema hii

"Hivi ndivyo nabii alivyoandika katika Maandiko zamani"

Tazama

"Ninawaambieni kitu muhimu" au "Sikiliza!' Neno 'tazama' hapa linatuchochea kuzingatia maelezo ya ajabu ambayo ifuatavyo. Lugha yako inaweza kuwa na njia ya kufanya hivyo.

jiwe la kona, mkuu na aliyechaguliwa na thamani

Maneno "mkuu" na "thamani" yanaelezea thamani ya "jiwe la msingi." AT "jiwe muhimu zaidi la kona, ambalo nimechagua."

jiwe la kona

Nabii alikuwa akiandika juu ya Masihi, ambaye ni Yesu.

1 Peter 2:7

jiwe lililokataliwa na wajenzi

Petro anasema nini nabii aliandika katika Maandiko zamani. "Jiwe" ni jiwe la msingi ambalo ni jiwe muhimu zaidi katika jengo hilo. Hii inahusu Yesu ambaye watu wengi walimkataa. AT "jiwe ambalo wajenzi walikataa."

jiwe la kikwazo na jiwe la kuwakumbusha

Petro anaeleza tena kile nabii aliandika zamani sana. Maneno haya mawili yanashiriki maana sawa. Pamoja wao wanasisitiza kwamba watu watachukuliwa na "jiwe" ambalo linamaanisha Yesu.

kutokutii neno

"kutokutii amri za Mungu

ambayo pia walichaguliwa

"ambao Mungu aliwachagua"

1 Peter 2:9

ninyi ni mbio iliyochaguliwa

Neno "ninyi" linamaanisha waamini katika Kristo.

alikuita nje

"alikuita utoke nje" au "alikuita ili ugeuke"

kutoka giza kwenda kwenye nuru yake ya ajabu

Hapa "giza" ina maana watu waliokuwa wenye dhambi na hawakujua Mungu. Na, "nuru" ina maana Mungu aliwafanya wamjue na kuanza kufanya kile kinachompendeza.

1 Peter 2:11

Wageni na watazamaji

Maneno haya mawili yanamaanisha kimsingi kitu kimoja. Petro anawatumia pamoja ili kusisitiza kuwa nyumbani kwao halisi ni mbinguni si duniani.

vita dhidi ya nafsi yako

"kutafuta kuharibu imani yako katika Mungu"

1 Peter 2:13

usiwe na uhuru wako

"usitumie uhuru wako"

kama kifuniko cha uovu

kwa udhuru wa kufanya mambo mabaya.

Wapende ndugu

"Wapendeni wakristo wenzenu"

1 Peter 2:18

Watumishi

Petro anazungumza na waumini ambao ni watumishi katika nyumba ya mtu.

wale wabaya

"watu wenye ukatili" au "watu wanaomaanisha"

ni sifa nzuri

"inafaa sifa" au "inampendeza Mungu"

1 Peter 2:21

Kwa hiyo uliitwa

Mungu amekuchagua wewe kuteseka kwa ajili yake.

Hakuna udanganyifu wowote uliopatikana kinywa chake

"Wala hakusema uongo."

Alipokuwa akitukanwa, hakuweza kumtukana.

Watu walipomtukana Yesu, hakuwaadhibu.

1 Peter 2:24

Yeye mwenyewe

Hii inamaanisha Yesu kwa msisitizo.

Alichukua dhambi zetu

Njia ambazo Yesu alikubali lawama na adhabu kwa dhambi za watu wengine.

Dhambi zetu

Tukio lolote la "yetu" na "sisi" linamaanisha Petro na waumini anaowandika.

Katika mwili wake kwenye mti

Hii inamaaniasha wakati watu walipo muweka Yesu msalabani.

Kwa mateso yake umeponywa

"Mungu amekuponya kwa sababu watu walimwumiza Yesu."

Ninyi nyote

Neno "Nyinyi" linamaanisha waumini Petro anawaandika.

mulikuwa mukitembea mbali kama kondoo muliopote.

Petro anawafananisha waumini na kupoteza kondoo kwa kutokuwa na upendo bila Kristo.

lakini sasa mumerejea kwa mchungaji na mlezi wa nafsi zenu

Kama vile kondoo watarejea kwa mchungaji wao, waumini pia wamerejea kwa Yesu ambaye hutoa na kuwahifadhi.

1 Peter 3

1 Petero 03 Maelezo kwa jumla

Muundo na mpangilio

Watafsiri wengine wametenga mistari ya ushairi mbele zaidi kuelekea kulia kuliko maandishi mengine ili yasomeke kwa urahisi. ULB hufanya hivi na ushairi ambao umenukuliwa kutoka Agano la kale katika 3:10-12

Dhana muhimu katika sura hii

"Mapambo ya nje"

Watu wengi wanataka kuonekana wazuri ili watu wawapende na kufikiri ni watu wazuri. Wanawake huwa makini sana kuonekana wazuri kwa kuvalia nguo nzuri na mapambo. Petero anasema kwamba kile mtu anafikiri na kusema na kutenda ni muhimu kwa Mungu kuliko jinsi anavyoonekana.

Umoja

Petero alitaka wasomaji wake kukubaliana na kila mmoja wao. Muhimu zaidi aliwataka wapendane na kuvumiliana.

Mifano muhimu za usemi katika sura hii

Mfano

Petero ananukuu Zaburi ambayo inamfafanua Mungu kama mtu aliye na macho, masikio na uso. Hata hivyo Mungu ni roho na kwa hivyo hawezi kuwa na macho, masikio ama uso wa kibinadamu. Lakini yeye anafahamu wafanyacho watu na huwadhibu watu waovu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

<< | >>

1 Peter 3:1

Kwa njia hii, ninyi ambao ni wake lazima munapaswa kuwasilisha kwa waume zenu

"Basi, wake, muwatii waume zenu."

kama wengine hawalitii neno

"ikiwa baadhi ya waume hawatii amri za Mungu" au "kama baadhi ya waumini hawaamini ujumbe kuhusu Kristo."

wataona

Maneno "wao" na "wao" yanataja waume.

1 Peter 3:3

Basi isifanyike

Neno "hilo" linamaanisha wake' kuwaheshimu waume zao.

1 Peter 3:5

Sasa wewe ni mtoto wake

Hii inamaanisha wake wa Kikristo ni kama watoto wa kiroho wa Sara kama wanafanya kama yeye.

1 Peter 3:7

Kwanjia ile ile

Kama vile wakezenu wanapaswa kukuheshimu.

kulingana na elimu kama mpenzi dhaifu wa kike

"tambua kwamba mwanamke ni mpenzi dhaifu"

Fanya hivi

Hapa "hivi" inahusu njia ambazo waume wanapaswa kuwatendea wake zao. "Heshimu amri hizi."

ili kwamba sala zako zisizuiliwe

Ili "kuzuia" ni kuzuia, au kuzuia sala za mtu kutotimizwa. AT "ili kwamba hakuna kitu kinachozuia sala zako."

1 Peter 3:8

Nyinyi wote

Sehemu tatu zilizopita zilishughulikia watumwa, wake, na waume. Sehemu hii inazungumzia makundi haya yote pamoja na waumini wengine wote.

Chuki

Hii ina maana ya kusema au kufanya kitu kibaya kwa mtu mwingine.

kinyume chake

"kwa njia tofauti"

wewe uliitwa

Mungu alikuita.

ili urithi baraka

"ili kwamba Mungu atakubariki"

1 Peter 3:10

Yule anayetaka kupenda maisha

Petro anasema nini mtunzi aliandika katika Maandiko zamani.

Anapaswa kuacha ulimi wake kwa uovu na midomo yake isiseme uongo

"acha uongo na kusema mambo maovu"

Nae aondoke mbali na yaliyo mabaya

"Nae aache kufanya mabaya"

Macho ya Bwana huwaona wenye haki

"Bwana anaona wenye haki" au "Bwana huwalinzi na huwajali wenye haki"

na masikio yake yanasikia maombi yao

"na anasikia sala zao"

uso wa Bwana ni kinyume

"Bwana hupinga"

1 Peter 3:13

Ni nani atakayekudhuru, ikiwa unataka mema?

Neno "wewe" linamaanisha waamini. AT "Hakuna mtu atakayekudhuru ikiwa unafanya mambo mema."

Usiogope kile wanachokiogopa. Msifadhaike.

Maneno haya mawili yanategemeana maana sawa na kusisitiza kwamba waumini hawapaswi kuwaogopa wale wanaowadhulumu. AT "Usiogope kile ambacho watu wanaweza kukufanyia."

1 Peter 3:15

Badala yake, mtekeleze Bwana Kristo katika mioyo yenu kama takatifu

Hapa "moyo" ina maana ya kuwa ndani ya mtu. AT "Badala yake, lazima uheshimu na kumpenda Bwana Kristo."

1 Peter 3:18

aliteseka kwa ajili yetu

Neno "sisi" linajumuisha msemaji, Petro na watazamaji.

Aliuawa katika mwili

Kristo alikuwa ameuawa kimwili na kufa kwenye msalaba wa Kirumi wa kuni. AT "Watu walimwua kimwili."

lakini alifanywa hai katika roho

Kristo alikuwa amefufuliwa kimwili kutoka kwa wafu au akafufuliwa tena kwa nguvu ya Roho Mtakatifu.

Katika roho, alienda na kuhubiri kwa roho ambao sasa gerezani

Baada ya kufa Kristo alikwenda mahali pa wafu na kuhubiri kwa roho za wale waliokufa kabla yake na walikuwa wakiwa mateka.

1 Peter 3:21

ambayo itawaokoa

"Nyinyi" inahusu waumini wote Petro alikuwa akizungumzia.

kuwasilisha kwake

"kuwasilisha kwa Yesu Kristo"

1 Peter 4

1 Petero 04 Maelezo kwa jumla

Muundo na mpangilio

Tafsiri zingine zimetenga mistari ya ushairi mbele zaidi kuelekea kulia kuliko maandishi mengine ili yasomeke kwa urahisi. ULB hufanya hivi na ushairi ambao umenukuliwa kutoka Agano la kale katika 4:18

Dhana muhimu katika sura hii

Watu wa mataifa wasiomcha Mungu.

Aya hii inatumia neno "Watu wa mataifa" kumaanisha watu wote wasiomcha Mungu na siyo Wayahudi. Haiwajumuishi Watu wa mataifa ambao wameisha kuwa Wakristo. Zambi za tamaa na ulevi na kuabudu sanamu zilikua tabia ya wasiomcha Mungu.

Kifo cha kishahidi

Ni wazi kwamba Petero anawazungumzia Wakristo wengi ambao wanapitia mateso mengi na wanakaribia kufa kwa ajili ya imani yao.

Maswala mengine ya utata katika tafsiri ya sura hii

"Na iwe" na "Hata mmoja asi" na "Mwache" na "Wacha hao"

Petero anatumia vifungu hivi vya maneno kuwaeleza wasomaji wake anachotaka wafanye. Ni kama maagizo ya kiamri kwa sababu anataka wasomaje wake wayatii. Lakini ni kama anamwambia mtu mmoja anachotaka na watu wengine wanaambiwa cha kufanya.

<< | >>

1 Peter 4:1

Kwa hiyo,

Neno hili linahitimisha mawazo ya Mtume Petro kwa kundi alilokuwa akiongea nalo.

Katika mwili

Katika mwili wake

Jivikeni wenyewe silaha za nia ileile

Neno "jivikeni wenyewe" linaelezea maaskari wanaotwaa silaha zao na kujiandaa kwa vita. Hapa inamaanisha kwamba waumini kuwa na dhamira katika mawazo yao ya kuteswa kama Yesu alivyoteswa. "Jiandae mwenyewe kutenda sawa na ilivyokuwa kwa Yesu"

wenyewe

Neno linafafanua kuhusu waumini katika sura ya kwanza.

1 Peter 4:3

ufisadi, nia mbaya, ulevi, ulafi, sherehe za kishenzi, na ibada za sanamu zenye machukizo

"dhambi za zinaa, tamaa mbaya, ulevi, sherehe za kinyama na ulevi, na ibada za sanamu ambazo ni chukizo kwa Mungu"

walio hai na waliokufa

Inamaanisha watu wote kama bado wako hai au kama wamekufa.

injili ilikuwa imehubiriwa

"Kristo aliihubiri habari njema"

ingawa wamekwisha kuhukumiwa katika miili yao kama wanadamu

"Ingawa Mungu aliwahukumu wakati walikuwa bado hai"

1 Peter 4:7

Mwisho wa mambo yote unakuja

"Karibuni Yesu atarudu na kukomesha mambo yote katika dunia hii

mwe na ufahamu ulio sahihi, na mwe na nia njema katika kufikiri kwenu

Maneno yote haya mawili yana maana ya jambo moja. Petro anayatumia kufafanua hitaji la kutafakari juu ya maisha wakati ukikaribia kuisha.

kufikiri kwenu

Neno linaelezea waumini wote

kwa kuwa upendo hautafuti kufunua dhambi za wengine

Petro anaelezea "upendo" kama vile mtu. Mtu anapopenda wengine hawatafanya juhudi kutafuta kama mwingine ametenda dhambi.

ukarimu

kuonyesha ukarimu kwa wageni na wasafiri

1 Peter 4:10

Kama kila mmoja wenu amepokea zawadi

"Mungu amempa kila mmoja wenu uwezo maalumu, na zaidi"

Na iwe kama mausia ya Mungu

"Na iwe kama maneno ya Mungu anayomwambia kunena"

Mungu apate kutukuzwa

"watu wote waweze kumtukuza Mungu"

1 Peter 4:12

Lakini kwa kadri mnavyozidi kupata uzoefu wa mateso ya Kristo, furahini

"Badasla yake, furahini kwamba mnatesekwa kwa mateso ambayo Kristo aliyasitahimili"

katika ufunuo wa utukufu wake

"wakati Yesu alivyoufunua utukufu wake"

Iwapo mmetukanwa kwa ajili ya jina la Kristo

"Kama watu wakiwatukana kwasababu mnamwamini Kristo"

Roho wa utukufu na Roho wa Mungu

Wote wanaelezea Roho Mtakatifu. "Utukufu wa Roho wa Mungu" au "Roho anayeufunua utukufu wa Mungu"

1 Peter 4:15

katika jina lile

"kwasababu watu wanamwita mkristo" au "kwasababu yeye ni mkristo"

1 Peter 4:17

nyumba ya Mungu

Neno hili linaelezea waumini, wale ambao wanamfuata Mungu kupitia Kristo.

Nini kitatokea kwa hao wasioitii injili ya Mungu?... nini kitakuwa kwa mtu asiye haki na mwenye dhambi?

Petro anatumia maswali kuwakumbusha watu jinsi itakavyokuwa vigumu kwa wenye dhambi wakati Mungu akiwahukumu. "...itakuwa ni matokeo ya kutisha kwao ambao hawaitii injili ya Mungu... kisha mtu asiye haki na mwenye dhambi atakutana na mateso ya kutisha wakati ujao"

1 Peter 5

1 Petero 05 Maelezo kwa jumla

Muundo na mpangilio

Watu wengi wa kale katika Mashariki ya karibu wangemalizia barua jinsi Petero anavyoimalizia hii.

Dhana muhimu katika sura hii

Mataji

Taji ambalo mchungaji Mkuu atapeana ni tuzo, kitu ambacho watu hupokea wakitenda mema. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#reward)

Mifano muhimu ya usemi katika sura hii

Simba

Wanyama wote wanawaogopa simba kwa sababu ya kasi na nguvu zao na pia wanakula karibu kila aina za wanyama. Pia wanakula binadamu. Shetani anataka kuwafanya watu wa Mungu kuwa waoga na kwa hivyo Petero anatumia mfano ya simba kufundisha wasomaji wake kwamba Shetani anaweza kudhuru miili yao. Lakini wakimwamini Mungu na kumtii, watakuwa watu wa Mungu na Mungu atawahudumia, (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-simile)

Babuloni

"Babuloni ilikuwa taifa ovu katika Agano la Kale. Taifa hilo liliharibu jiji la Yerusalemu na likawateka Wayahudi kutoka maboma yao na wakawatawala. Petero anatumia Babuloni kama mfano ya taifa ambalo lilikuwa linawatesa Wakristo aliokuwa anawaandikia. Huenda aliamaanisha Yerusalemu kwa sababu Wayahudi walikuwa wanawatesa sana Wakristo ama aliashiria Roma kwa sababu Warumi walikuwa wanawatesa Wakristo. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#evil and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

__<< | __

1 Peter 5:1

wazee kati yenu

Neno "wewe" linamaanisha waumini katika Kristo.

ambayo itafunuliwa

"Kwamba Mungu atafunua."

Kwa hiyo

"Kwa sababu hii"

kundi la Mungu

Hii inalinganisha kanisa na kundi la kondoo.

Angalia

"tahadhari" au "huwa"

Usitende kama bwana

"Usitende kama bosi mwenye ukatili"

Wakati Mchungaji Mkuu akifunuliwa

"Wakati Yesu, ambaye ni kama mchungaji wetu mkuu, anaonekana." (UDB)

taji yenye utukufu usio na nguvu

Hapa taji inawakilisha thawabu iliyopatikana baada ya ushindi. AT "tuzo ya utukufu ambayo itaendelea milele."

1 Peter 5:5

Ninyi nyote

Hii inahusu waumini wote, sio tu wanaume wadogo.

jifunge kwa unyenyekevu

"wanapaswa kutenda kwa unyenyekevu kwa kila mmoja." (UDB)

chini ya mkono wa nguvu wa Mungu

"chini ya nguvu za Mungu"

Kutoa wasiwasi wako wote juu yake

"Mwamini kwa kila kitu kinachokupa wasiwasi wewe" au "Muache yeye ashughulikie mambo yote yanayo kusumbua"

anakujali

"anahusika na wewe"

1 Peter 5:8

kama simba angurumaye

Petro anafananisha shetani na simba ili kusisitiza kwamba shetani ni mkatili na mkali.

akizunguka karibu

"kutembea karibu" au "kutembea karibu na kuwinda"

Simama dhidi yake

"Mshinde"

Katika ulimwengu

"katika maeneo mbalimbali ulimwenguni"

1 Peter 5:10

kwa muda mfupi

kwa muda mfupi

Mungu wa neema zote

"Mungu ambaye ni mwema kabisa"

aliyekuita kwenye utukufu wake wa milele katika Kristo

"ambaye alituchagua kushiriki utukufu wake wa milele mbinguni kwa sababu tunajiunga na Kristo" (UDB)

kamili wewe

"kukurejesha"

kuanzisha wewe

"kukuweka salama"

Utangulizi wa 2 Petero

Sehemu ya 1: Maelezo kwa jumla

Muhtasari wa kitabu cha 2 Petero

  1. Utangulizi (1:1-2)
  2. Kukumbusha kuishi maisha mema kwa sababu Mungu ametuwezesha (1:3-21)
  3. Onyo kuhusu walimu wa uongo (2:1-22)
  4. Kutia moyo kujiandaa kwa ujio wa pili wa Yesu (3:1-17)

Nani aliandika kitabu cha 2 Petero?

Mwandishi anajitambulisha kama Simoni Petero. Petero alikuwa mtume. Pia aliandika 1 Petero. Kuna uwezekano Petero aliandika barua hii akiwa gerezani Roma muda mfupi kabla ya kifo chake. Petero aliita barua hii kama barua ya pili na kwa sababu hiyo tunaiorodhesha baada ya 1 Petero. Aliandikia barua hii kwa hadhira moja ya barua yake ya kwanza. Kuna uwezekano hadhira hii ilikuwa ni Wakristo waliotawanyika katika inchi za Asia Ndogo.

Kitabu cha 2 Petero kinahusu nini?

Petero aliandika barua hii kuwapa moyo waumini waishi maisha mema. Aliwaonya kuhusu walimu waongo waliosema Yesu alikuwa anachukua muda mrefu kurudi. Aliwaambia Yesu hakuchelewa kurudi ila ni Mungu alikuwa anawapatia watu muda wa kutubu ili waokolewe.

Kichwa cha kitabu hiki kinastahili kutafsiriwa namna gani?

Watafsiri wanaweza kukiita kitabu hiki kutumia jina lake la kitamaduni, "2 Petero" ama "Petero wa Pili" ama wanawezatumia kichwa kinachoeleweka zaidi kama, "Barua ya Pili kutoka kwa Petero" ama "Barua ya pili aliyoandika Petero" (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-names)

Sehemu ya 2: Dhana muhimu za kidini na kitamaduni

Ni watu gani Petero aliwakemea?

Labda watu Petero aliwakemea ni watu waliojulikana kwa jina la Wagnostiki. Walimu hawa waliharibu mafundisho ya maandiko matakatifu kwa manufaa yao wenyewe. Waliishi maisha maovu na wakafundisha watu kuishi hivyo .

Nini maana ya kwamba Mungu aliongoza maandiko?

Mafundisho ya Maandiko ni muhimu sana. 2 Petero inawasaidia wasomaji kuelewa kwamba ingawa kila mwandishi wa maandiko ana njia yake ya kipekee ya kuandika, Mungu ndiye mwandishi wa kipekee wa maandiko. (1:20-12)

Sehemu ya 3: Maswala muhimu ya tafsiri

Umoja na wingi wa "Wewe" na "Nyinyi"

Katika kitabu hiki, neno "mimi" linaashiria Petero. Pia neno "Nyinyi" linaashiria hadhira ya Petero. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-exclusive and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-you)

Ni maswala gani muhimu katika maandiko ya kitabu cha 2 Petero?

Katika mistari ifuatayo, matoleo ya kisasa ya Bibilia yanatofautiana na matoleo ya kale. Toleo la ULB lina masomo ya kisasa na linaweka masomo ya zamani kama maelezo ya chini. Kama tafsiri ya Bibilia iko katika eneo kwa ujumla, watafsiri wanapaswa kuzingatia masomo ya matoleo hayo. Kama si hivyo, wanapaswa kufuata masomo ya kisasa.

(See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/jit.html#translate-textvariants)

2 Peter 1

2 Petero 01 Maelezo kwa jumla

Dhana muhimu katika sura hii

Kumjua Mungu

Kumjua Mungu inamaanisha kumilikiwa naye ama kuwa na uhusiano naye. Hapa "ujuzi" ni zaidi ya kumjua Mungu na akili. Ni ujuzu unaomfanya Mungu kumuokoa mtu na kumpa neema na amani. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#know)

Kuishi maisha ya ya kumcha Mungu

Petero anafundisha kwamba Mungu amewapa waumini yote wanayohitaji kuishi maisha ya kumcha Mungu. Kwa hivyo waumini wafanye kila waezalo kumtii Mungu zaidi. Waumini wakiendelea kufanya hivyo watakuwa imara na wenye manufaa kupitia uhusiano wao na Yesu. Lakini waumini wasipoendelea kuishi maisha ya kumcha Mungu, watakuwa ni kama wamesahau walichofanyiwa na Mungu kupitia kwa Kristo kuwaokoa. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#godly and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#save)

Maswala mengine ya utata ya kutafsiri katika sura hii

Ukweli wa Maandiko

Petero anafundisha kwamba unabii wa maandiko haukutolewa na binadamu. Roho Mtakatifu alifunua ujumbe wa Mungu kwa watu waliouandika kwa kitabu. Petero pia na Mitume wengine hawakubuni hadithi walizowapa watu kuhusu Yesu. Walishuhudia chenye Yesu alifanya na wakamsikia Mungu akimwita Yesu mwanawe.

| >>

2 Peter 1:1

Simon Petro

"Kutoka Kwa Simoni Petro." Lugha Yako inaweza kuwa na namna fulani ya kumtambulisha mwandishi wa barua. Mimi Simon Petro niliandika barua hii.

Mtumwa na Mtume waYesu Kristo

Petro anaongelea mtazamo wake wa kuwa mtumwa wa Yesu Kristo. Pia alipewa nafasi na mamlaka ya kuwa mtume wa Kristo

Kwa wale

Petro anaonekana kuwaandikia waumini wote watakaosoma waraka huu. Kwenu waumini.

Tumepokea

Sisi mitume tumepokea

Neema iwe kwenu

Neno "ninyi" linamaanisha waumini wote kwa ujumla

Yesu Bwana wetu

Yesu Bwana wa waumin na Mitume

Neema na iwe kwenu;amani iongezeke kupitia maarifa ya Mungu na Yesu Bwana wetu.

Upole wenu na amani uongezeka kwa sababu mnamjua Mungu na Yesu Bwana wetu.

2 Peter 1:3

Aliyetuita

Kwanza Mungu alitufikia. "Sisi" Neno hili linamanisha Petrop pamoja na wasikilizaji wake.

Kwa ajili ya uzuri wa utukufu wake

"kwa njia ya heshima yake na uzuri wa maarifa"

Kwa njia hii alitutumainishi ahadi kuu za thamani

"Ahadi za thamani za Mungu zilikuja njia ya heshima na uzuri wa maarifa"

asili ya Mungu

"tabia ya ukamilifu wa Mungu"

kwa kadiri tunavyoendelea kuachc uovu wa dunia

kadiri unavyoendelea kuziacha tamaa mbaya za dunia."

2 Peter 1:5

Kwa sababu hii

Kwa sababu ya kile ambacho Mungu amefanya

maarifa

"uzuri wa maarifa"

Kwa sababu ya uzuri maarifa

kwa kutumia uzuri wa maarifa uongeze ufahamu

kupata upendo wa ndugu

kuwa wapole kwa sisi kwa sisi

2 Peter 1:8

mambo haya

haya mambo ni:- imani, uzuri, maarifa, kiasi, uvumilivu, utauw, upendo wa ndugu, na upendo.

"Ninyi hamtakuwa tasa au msiozaa matunda"

mtazaa matunda

yeyote asiyekuwa na mambo haya

mtu yeyote asiyekuwa na mambo haya

huyaona mabo ya karibu tu, yeye ni kipofu

usemi huu unamfananisha mtu anayefikiria mambo ya duniani tu kuwa yako vizuri mbele yake, kama mtu asiye na macho.

2 Peter 1:10

kwa hiyo

Neno "kwa hiyo" linaanzisha mwitikio wa waumini kwa kile kilichosemwa mapema.

kujihakikishia uteule na wito kwa ajili yenu

Neno " wito" linamaanisha mwaliko wa ujula waMungu kwa watu wote. Neno "uteule" linamaanisha watu maalumu ambao Mungu amewchagua. Maneno haya mawili yana maana sawa.

hamtajikwaa

hamtashindwa kiroho na katika tabia njema

2 Peter 1:12

Kwa hiyo

Mwandishi anataka kutengeneza maelezo ambayo yanatokana na kile alichoandiaka mwanzoni.

Nitakuwa tayari kuwakumbusha mambo haya

Petro anaonyesha kuwa ataendelea kuwakumbusha waumini jinsi ya kumfuata Kristo

juu ya mabo haya

jinsi waumini inavyowapasa kukua katika imani

kuwaamsha

huu ni ufafanuzi unaomaanisha "kuwaandaa ili wawe tayari"

nimo katika hema hii

Haya maelezo yanaytumika badala ya "kwa sababu bado ninaishi"

Nitajitahidi kwa bidii kwa ajili yenu ili mkumbuke mambo haya

"Ntatumia juhudi zangu kuwafundish mambo haya ili muyakumbuke"

Nitaiondoa hema yangu

huu nu ufafanuzi wa "Nitakufa"

Baada yakuondoka Kwangu

Maelezo haya yanaonyesha "baada ya kufa kwangu"

2 Peter 1:16

Pale sauti iliposikika toka katika utukufu mkuu

Petro anamaanisha yeye mwenyewe na yule mwanafunzi mwingine, Yakobo, na Yohana waliposikia ile sauti ya Mungu.

Kwa kuwa sisi hatukufuata hadithi zilizoingizwa kwa ustadi

Kwa kuwa sisis mitume hatukufuata hadtibzilizotengenezwa kwa ustadi

Yetu

waumini wote ikijumuisha sisi mitume

Pale tulipokuwa naye kwenye ule mlima matakatifu

Petro anamaanisha wakati ule Yesu alipobadilika sura yake ikang'aa mbele ya Petro, Yakobo na John (Tazama Mathayo)

2 Peter 1:19

Tunalo hili neno la unabii lililothibitika

Perto anamaanisha wale Mitume. Mitume wnaujumbe kutoka kwa malaika ambao wanajua kuwa ndiyo ukweli kutoka kwa Mungu

Ambalo kwalo mwafanya vyema kulitekeleza

Petro anawaelekeza waumini kuwa na utayari kwa jumbe za kinabii

Ni kama taa ing'aayo gizani mpaka kunapokucha

Ujumbe wa kinabii umelinganishwa na taa inayotoa Mwanga gizani mpaka mwanga unapowadia asubuhi.

Na nyota za mawio zionekanapo katika mioyo yenu

Nyota ya asubuhi ni Kristo anayekuja kuishi kwenye mioyo yetu.

isipokuwa wanadamu waliwezeshwa na Roho mtakatifu aliyeongea toka kwa Mungu

Roho mtakatifu aliwaongoza watu hawa, kwa hiyo waliongea ambacho Mungu alitaka waongee.

2 Peter 2

2 Peter 02 Maelezo kwa ujumla

Dhana muhimu katika sura hii

Nyama

"Nyama" ni mfano ya asili ya dhambi ya mtu. Siyo sehemu ya kimwili ya binadamu iliyo na dhambi. "Nyama" inawakilisha asili ya binadamu inayokataa vitu vyote vya uungu na kutamani vitu vya kidhambi. Hii ndiyo hali ya binadamu wote kabla ya kumpokea Roho Mtakatifu kwa njia ya kumwamini Yesu Krsito. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#flesh)

Mafundisho fiche

Kuna ulinganifu katika 2:4-8 ambao ni mgumu kuelewa iwapo Agano la kale halijatafsiriwa. Maelezo zaidi ni muhimu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

<< | >>

2 Peter 2:1

Manabi wa uongo walikuja kwa Israeil, na walimu a uongo watakuja kwenu

Kama ile manabii wa uongo walivyokuja wakiidanganya Isreli, vivyo hivyo walimu wa uongo watakuja wakidanganya uongo juu ya Kristo

Ukengeufu

Haya ni maoni yaliyo kinyume na mafunisho ya Kristo na ya Mitume

Bwana aliyewanunua

Yesu ndiye Bwana aliyelipa kwa ajili ya dhambi za watu wote kwa njia ya kifo chake, na kuzikwa kwake na ufufuo.

nja za aibu

Neno "zao" linawakilisha manabii na walimu wa uongo" jinsi matendo yao yalivyo ya zinaa iliyokidhiri.

2 Peter 2:4

Maana Mungu hakuwaacha malaika waliokengeuka

Hii inaanzisha Mpangilio wa sentensi zinazoanza na "kama"

bali aliwatupa kuzimu ("Tartarus)

"Tartarus

ili wafungwe minyororo mpaka hukumu itakapowajilia

Mungu atawaweka katika gereza wakisubiri hukumu ya mwisho

Wala Mungu hakuuvumilia ulimwengu wa zamani...wakati alipoachilia gharika juu yaulimwengu ulioasi

Mungu aliuhribu ulimwengu wa zamani na watu waasi kwa gharika

Mungu aliihukumu miji ya Sodoma na Gomorra kiasi cha kuwa majivu

Mungu alitumia moto kuwaharibu watu wasi mcha Yeye katika miji ya Sodoma na Gomora

bali alimhifadhi Nuhu

Mungu alimwokoa mtu wa haki Nuhu katika gharika

ili iwe mfano kwa ajili ya watu waovu katika siku za usoni

kama vile Sodoma na Gomora ilivyoharibiwa kwa moto katika siku za usoni Mungu atawaharibu katika ziwa la moto.

2 Peter 2:7

alimwokoa Ltu mtu wa haki

Mungu alimwokoa Lutu aliyeishi maisha ya tabia njema

akitesa nafsi yake kwa ajili ya yale alyosikia na kuyaona

Lutu aliendelea kuteseka na kuhrasiwa na tabia za anasa za wenyeji wa Sodoma na Gomora

tabia chafu za wsiofuata sheria

"anasa na tabia inayoharibika ya watu waliovunja sheria ya Mungu"

mtu wa haki

Hii inamaanisha Lutu mtu wa haki

watu wa Mungu

"watu wanaomtii Mungu"

alikuwa akitesa roho yake

Aliusumbua utu wake wa ndani

jinsi ya kuwavumilia waovu kwa ajil ya hukumu skatika siku ya mwisho

Watu wasio haki hawataiepuka hukumu ya Mungu. Watakapokufa watakataliwa mpaka siku ya hukumu

2 Peter 2:10

kwa hakika huu ndio ukweli

Neno "huu" linamaanisha Mungu kuwalinda watu wasio haki gerezani mpaka siku ya hukumu.

wale wanaoendelea kuishi katika tamaa za mwili huu na kuyadharau mamlaka

Watu wasio haki wanaoendela kuishi katika tamaa ya mwilii na kuwachukia viongozi wao au watawala wao.

mwili

Neno "mwili" linamaanisha ubinadamu katika dhambi ya asili ya mwanadamu

wana ujasiri katika dhamiri zao

Neno "dhamiri" linamaanisha wale wanaoendelea katika uharibifu wa tamaa katika dhambi zao za asili na hawaheshimu malaika na mamlaka ya kiroho

Hwaogopi kuwakufuru watukufu

Wasio haki hawaogopi kuwachokoza na kuwanenea maovu malaika

malaika wana uwezo na nguvu kuliko wanadamu

Malaika wana nguvu za mwili na wa mamalka kuliko wanadamu

Lakini hawawezi kuleta hukumu dhidi yao kwa Bwana

"lakini malaika hawaleti humu iumizayo dhidi ya hawa watu kwa Bwana"

2 Peter 2:12

hawa wanyama wasio na akili

Kama vile wanyama wasivyoweza kueleza kwa mantiki, vivyo hivyo hawa watu hawaezi kuwa na mantiki, "Hawa walimu wa uongo wako kama wanyama wasio na akili"

Hawajui wanachotukana

Huongea uovu ambao hawaujui

wataangamizwa

Mungu atwaangamiza watu hawa

Wataumizwa kwa ujira wa maovu yao

"Wanachofikiri kuwa ni kizuri kwao, kiuhalisia ni kibaya kwao"

Wamejaa uovu na uchafu

Neno "uchafu" na "uovu" vinamaanisha maana moja. Waalimu wa uongo hufedhehesha na kutahayarisha amabavyo ni sawa na uchafu na uovu ambavyo mtu hawezi kviondoa

hufurahia udanganyifu wanaposherehekea na wewe

huendele katika furaha ya kuwadanganya watu wasio hatia na katika macho yao hawaonyeshi hatia

macho yao yamefunikwa na uzinzi, hwatosheki kutenda dhambi

"wanatamani kila mwanmke wanayemuona na kamwe hawatosheki"

wana mioyo iliyofunzwa kujaa tamaa

" inawakirisha mtu kama kamili, alifunzwa katika mawazo na na mattendo ya uchoyo. wanatamani utajiri na miliki isiyo haki.

2 Peter 2:15

Wameiacha njia ya kweli, wamepotoka na wamefuata...

"walimu wa uongo .wameiacha...wamepotoka..wamefuata". Walimu wa uongo wamekataa kumtii Mungu kwa kukataa kilicho sahihi

aliyependa kupata malipo yasiyo haki

alipokokea malipo ya anasa na yenye matendo ya dhambi

Lakini alikemwa kwa ajili ya ukosaji wake

alionywa vikali kwa kutokutii kwake

alizuia wazimuwa nabii

Mungu alitumia punda kuzuia upumbavu wa nabii

2 Peter 2:17

Watu hawa ni kama chemichemi zisizo na maji

Kama vile chemichemi zilizokauka na hazitoi maji kwa ajili ya maisha ya kawaida, vivyo hivyo mafundisho yao hayawaongozi watu katka maisha ya kiroho. Ni eneo la uongo kuwafariji waatu, kisima kikavu

Ni kama mawingu yanayotoweshwa na upepo

Mawingi mengine hubeba mvua. Mvua hii huleta maji yanayokuza au maji yagharikishayo. Hawa watu ni kama hayo mawingu yanayobeba uharibifu.

Huongea kwa majivuno matupu

Hotuba zao ni za kujivuna zisizo na maana.

Huangusha watu kwa tamaa ya mwili

Wanawavuta watu ili waingie katika dhambi ya mwili na matendo ya anasa.

Huwaahidi watu uhuru wakati waowenyewe ni watumwa wa dhambi ya ufisadi.

Huahidi uhuru wa uongo, uhuru unaowapeleka watu kutendda dhambi. huu ni utumwa wa dhambi.

Maana mwanadamu hufanywa kuwa mtumwa kile kinachmtawala

Mwanadamu hufanya kwa tamaa mabo yale anayopungukiwa kiasi

Huwalaghai watu wanaojaribu kuwakimbia wale waishio katika ukosji

Hujaribu kuwaangamiza watu ambao ni wapya katika imani.

2 Peter 2:20

Yeyote ajiepushaye na uchafu wa ulmwengu kwa kutumia maarifa ya Bwana na mwokozi Yesu Kristo

Mtu yeyote ambaye amempokea Bwana na Mwokozi Yesu Kristo na kugeuka kutoka kwenye uchafu na maisha yasyo matakatifu.

Hali yake huwa mbaya kuliko ile ya mwanzo

Ni wabaya zaidi kwa sababu wana maarif ya maisha matakatifu na wamechagua kurudi kwenye maisha ya dhambi

kama wasingeifahamu njia ya haki

Maisha ya yanayompendza Mungu.

amri takatifu walizopewa

Sheria za Mungu na amri za Mungu ambazo wamepewa wangejua namna ya kuishi kwa ajili ya Mungu

Mithali hii...mbwa huyarudia matapishi yake, Na nguruwe aliyeoshwa hurudi tena kwenye matope."

Ni usemi wa busara unaowalinganisha wale wanaoijua kweli lakini wanrudia maisha ya uasi. "Mbwa huyarudia matapishi yake" imenukuliwa toka Mithali 26:11. Katika namna yeyote maana yake inabaki kuwa "mnyama hawezi kufundishika ili asijnajisi mwenyewe"

2 Peter 3

2 Petero 03 Maelezo kwa jumla

Dhana muhimu katika sura hii

Moto

Watu hutumia moto mara nyingi kuharibu vitu ama kukifanya kitu kiwe safi kwa kuondoa uchafu na vitu visivyofaa. Kwa hivyo Mungu anapowadhibu waovu ama kuwatakaza watu wake, huwa inalinganishwa na moto. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#fire)

Siku ya Bwana

Wakati kamili wa kurudi kwa Bwana itakuwa mshangao kwa wengi. Hii ndiyo maana ya tashbihi "kama mwizi wa usiku". Kwa sababu ya haya Wakristo wanafaa wajiandae kwa ajili ya kurudi kwake Bwana. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#dayofthelord and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-simile)

__<< | __

2 Peter 3:1

Maelezo ya ujumla

Petro anaanza kuzungumza kuhusu siku za mwisho

kukuamsha katika akili

Petro anasema kwa kusababisha wasomaji wake kufikiri kuhusu mambo haya kama alikuwa anawaamsha kutoka kwenye usingizi. "kuwasababisha kufikiri kwa mawazo safi"

maneno yaliyosemwa kabla na manabii watakatifu

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "maneno ambayo manabii watakatifu walisema wakati uliopita"

amri ya Bwana wetu na mwokozi kwa kutumia mitume

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "amri ya Bwana wetu na Mwokozi, ambayo mitume wenu waliwapa"

2 Peter 3:3

Ujue ili kwanza

"Ujue hili kama jambo la muhimu sana."

wakienenda saswasa na matakwa yao

Hapa neno "matakwa" urejea kwa tamaa mbaya ambazo ziko kinyume na mapenzi ya Mungu. "kuishi sawasawa na tamaa zao mbaya"

kuendelea

kitendo, tenda

Iko wapi ahadi ya kurudi kwake?

Wabishi wanauuliza swali la utupu kusisitiza kuwa hawaamini kuwa Yesu atarudi. Neno "ahadi" urejea kwa kutimizwa kwa ahadi kuwa Yesu atarudi. "Ahadi ya kuwa Yesu atarudi sio kweli! Hatarudi!

Baba zetu walikufa

Hapa "Baba" urejea kwa mababu walioishi zamani. "Walikufa" ni lugha ikimaanisha walikufa.

vitu vyote vilikuwa hivyo tangu mwanzo wa uumbaji.

Wabishi wanajadili kwamba hakuna chochote katika ulimwengu kimeweza kubadilika, haiwezi kuwa kweli kwa Yesu kurudi.

tangu mwanzo wa uumbaji.

Hii inaweza kutofasiriwa kama kikundi cha maneno ya kitenzi. "Kwani Mungu aliumba ulimwengu"

2 Peter 3:5

mbingu na nchi vilianza... zamani, kwa amri ya Mungu

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "Mungu alianzisha mbingu na nchi... zamani kwa neno lake"

vilianza kutokana na maji na kupitia maji

Hii inamaanisha kuwa Mungu alisababisha ardhi kutoka kwenye maji, kukusanya maji kwa pamoja kufanya ardhi ionekane.

kupitia neno lake

Hapa "neno lake" urejea kwa neno la Mungu na maji

ulimwengu kwa kipindi hicho, ikiwa imejaa maji, iliharibiwa

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "Mungu aliujaza ulimwengu na maji kwa kipindi hicho na kuuharibu"

mbingu na dunia zimetunzwa kwa neno hilo hilo kwa ajili ya moto.

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "Mungu kwa neno lile lile, ametunza mbingu na nchi kwa ajili ya moto."

kwa neno hilo hilo

Hapa "neno" usimama kwa Mungu, atakaye toa neno.

Vimehifadhiwa kwa ajili ya siku ya hukumu

Hii kusemwa katika kauli tendaji na kuanza sentensi mpya. "Anawatunza kwa ajili ya siku ya hukumu"

kwa ajili ya siku ya hukumu na maangamizi ya watu wasio wa Mungu

Hii inaweza kusemwa pamoja na maneno ya kitenzi. "kwa siku wakati anapohukumu na kuharibu watu wasio wa Mungu"

2 Peter 3:8

Hii haiwezi kuchenga ujumbe wako

"Hauwezi kushindwa kuelewa hili" au "Usipuuze hii"

kwamba siku moja kwa Bwana ni kama miaka elfu moja

"kwamba kutoka kwa mtazamo wa Bwana, siku moja nia kama miaka elfu moja"

Si kwamba Bwana anafanya pole pole kutimiza ahadi

"Bwana si kwamba anafanya pole pole kutimiza ahadi zake"

kama inavyofikiriwa kuwa

Baadhi ya watu wanafikiri kuwa Bwana si kwamba anafanya pole pole kutimiza ahadi zake kwa sababu mtazamo kuhusu wakati ni tofauti na Mungu.

2 Peter 3:10

hata hivyo

Ijapokuwa Bwana ni mvumilivu na anataka watu watubu, hakika atarudi na kuleta hukumu.

siku ya Bwana itakuja kama mwizi

Petro anazungumza juu ya siku ambayo Mungu atamhukumu kila mmoja kama mwizi anayekuja pasipo kutegemewa na kuwashtusha watu.

Mbingu itapita kwa kupaza kelele

"Mbingu zitapita"

Vitu vitateketezwa kwa moto

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "Mungu atateketeza kwa moto"

Vitu

Maana zinazowekana ni 1) vitu vya mbinguni kama vile jua, mwezi, na nyota au 2) vinavyofanya mbingu na nch, kama vile mchanga, hewa, moto na maji.

nchi na matendo yatafunuliwa

Mungu ataiona dunia yote na matendo yote ya kila mmoja, na atahukumu kila kitu. Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "Mungu ataiweka wazi nchi na kila kitu watu walichofanya."

2 Peter 3:11

Sentensi unganishi

Petro anaanza kwa kuwaambia wakristo namna watakavyo ishi wakati wanasubiri siku ya Bwana.

Kwa kuwa vitu vyote vitateketezwa kwa njii hii.

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "Tangu Mungu atahukumu mambo haya yote katika njia hii"

je utakuwa mtu wa aina gani?

Petro anatumia swali la kejeli kusisitiza kile atakachosema badae, kwamba "wanapaswa kuishi maisha ya utakatifu na utaua" "unajua ni aina gani ya watu wanapaswa kuwa"

mbingu itateketezwa kwa moto, na vitu vitayeyushwa katika joto kali

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "Mungu ataangamiza mbingu kwa moto, na ataviyeyusha

sehemu ambayo watakatifu wataishi

Petro anazungumza juu ya "utakatifu" kama ilivyokuwa kwa mtu. HIki ni kirai cha watu anaishi au sehemu ya watu watakao ishi kwa utakatifu.

2 Peter 3:14

jitahidi kuwa makini na kutolaumika na kuwa na amani pamoja naye

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "jitahidi kuishi katika njia ili kwamba Mungu asikute doa na kulaumiwa na kuwa na amani na yeye na kila mmoja"

doa na kutolaumiwa

Maneno "doa" na "kutolaumiwa" kimsingi umaanisha kitu kile kile na kusisitiza maadili ya usafi."usafi kamili"

doa

Hii usimama kwa ajili ya "kosa"

zingatia uvumilivu wa Bwana wetu katika wokovu

Kwa sababu Bwana ni mvumilivu, siku ya hukumu bado haijatokea. Hii uwapa watu fursa ya kutubu na kuokolewa, kama alivyo elezea katika 3:8. "Pia, nafikiri kuhusu uvumilivu wa Bwana wetu kama kukupa fursa ya kutubu na kuokolewa"

kutokana na hekima ambayo alipewa.

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "kutokana na hekina ambayo Mungu alimpa"

Paulo anaongelea hayo yote katika barua zake,

"Paulo anaongelea katika barua zake uvumilivu wa Mungu kuwaongoza katika wokovu"

kuna vitu ambavyo ni vigumu kuvielewa.

Kuna vitu katika barua za Paulo ambavyo ni vigumu kuvielewa.

Watu wasio na adabu na uimara wameviharibu vitu hivyo

watu wajinga na wasio na uimara hutofasiri vibaya vitu katika barua za Paulo kwamba ni ngumu kuelewa.

Wajinga na uimara

"Wasio wa kawaida na legarega" Hawa watu hawajafundishwa namba ya kutofasiri maandiko na hawajafanywa imara katika ukweli wa injili.

Kuelekea maangamizi yao.

"matokea yake ni maangamizi yao"

2 Peter 3:17

Sentensi unganishi

Petro anamalizia kuwaelekeza wakristo na kumalizia barua yake.

Hivyo, wapendwa kwa kuwa mnayafahamu hayo.

"Hayo" urejea kwa ukweli kuhusu uvumilivu wa Mungu na mafundisho ya walimu wa uongo.

jilindeni wenyewe

"jilindeni wenyewe"

ili kwamba msipotoshwe na udanganyifu wa walaghai

Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "ili kwamba walaghai wasiwapotoshe kwa maneno yao ya udaganyifu

msipotoshwe...udanganyifu

Kushawishiwa kuto mtii Mungu kunaongelewa kama kuondolewa katika njia sahihi ya kufuata. Udanganyifu na mafundisho ya uongo yanaongelewa kama watu wanaoweza kumoongoza mtu nje ya njia sahihi.

kupoteza uaminifu wako

Uaminifu unaongelewa kama kitu cha kumiliki ambacho wakristo wanaweza kukipoteza. "wewe acha kuwa mwaminifu"

mkue katika neema na ufahamu

"kuongozeka katika neema na ufahamu"

neema na ufahamu wa Bwana na mwokozi Yesu Kristo

Unaweza kutofasiri "neema" na 'ufahamu" kutumia maneno kitenzi. Ona utakavyo tofasiri maneno hayo hayo katika 1:1 na 1:8 na 2:20. "kuwa na uzoefu zaid na zaid na Bwana na Mwokozi Yesu Kristo kukutenda wema wewe, na kwamba unapata kumjua yeye vizuri na vizuri"

Utangulizi wa 1 Yohana

Sehemu ya 1: Utangulizi wa Ujumla

Maelezo ya Kitabu cha 1 Yohana

  1. Utangulizi (1:1-4)
  2. Kuishi Kikristo (1:5-3:10)
  3. Amri ya kupendana (3:11-5:12)
  4. Hitimisho (5:13-21)

Nani aliandika Kitabu cha 1 Yohana?

Kitabu hiki hakitaji mwandishi. Hata hivyo, tangu wakati wa Kikristo wa kwanza, Wakristo wengi wamefikiri kwamba Mtume Yohana ndiye aliyekuwa mwandishi. Yeye pia aliandika Injili ya Yohana.

Je, kitabu cha 1 Yohana kinahusu nini?

Yohana aliandika barua hii kwa Wakristo wakati ambapo walimu wa uongo walikuwa wakiwasumbua. Yohana aliandika barua hii kwa sababu alitaka kuzuia waumini wasitende dhambi. Alitaka kuwalinda waumini dhidi ya mafundisho ya uongo. Na alitaka kuwahakikishia waumini kwamba walikuwa wameokolewa.

Je, kichwa cha kitabu hiki kinapaswa kutafsiriwaje?

Watafsiri wanaweza kuchagua kuita kitabu hiki kwa kichwa chake cha jadi, "1 Yohana" au "Yohana wa Kwanza." Au wanaweza kuchagua kichwa cha wazi, kama "Barua ya Kwanza Kutoka kwa Yohana" au "Barua ya Kwanza Aliyoandika Yohana." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-names)

Sehemu ya 2: Dhana muhimu za Kidini na za Kitamaduni

Ni watu wapi ambao Yohana alizungumza dhidi yao?

Watu ambao Yohana alizungumza dhidi yao inawezekana kwamba walikuwa wale ambao wangejulikana kama Wagnostiki. Watu hawa waliamini kwamba dunia ni uovu. Kwa kuwa waliamini kwamba Yesu alikuwa wa kiungu, walikanusha kwamba alikuwa mwanadamu kweli. Hii ni kwa sababu walidhani Mungu hawezi kuwa mwanadamu kwa sababu mwili ni uovu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#evil)

Sehemu ya 3: Masuala muhimu ya Tafsiri

Maneno "kubaki" na "kuishi" na "kukaa" yana maana gani katika 1 Yohana?

Yohana mara nyingi alitumia maneno "kubaki," "kuishi," na "kukaa" kama sitiari. Yohana alizungumzia muumini kuwa mwaminifu zaidi kwa Yesu na kumjua Yesu vizuri ikiwa neno la Yesu "lilibaki" ndani ya muumini huyo. Pia, Yohana alizungumzia mtu aliyejiunga kiroho na mtu mwingine kana kwamba mtu "aliyebaki" katika mtu mwingine. Wakristo wanasema "kubaki" katika Kristo na kwa Mungu. Baba anasemekana "kubaki" ndani ya Mwana, na Mwana anasemekana"kubaki" ndani ya Baba. Mwana anasemekana "kubaki" katika waumini. Roho Mtakatifu pia anasemekana "kubaki" ndani ya waumini.

Watafsiri wengi wataona kuwa ni vigumu kuwakilisha mawazo haya katika lugha zao kwa njia hiyo hiyo. Kwa mfano, Yohana alitaka kueleza wazo la Mkristo kuwa pamoja na Mungu kiroho wakati alisema, "Yeye asemaye anakaa katika Mungu" (1 Yohana 2: 6). UDB inasema, "Ikiwa tunasema kuwa sisi tuna umoja na Mungu," lakini watafsiri mara nyingi wanapaswa kutumia maneno mengine ambayo yanawasilisha mawazo haya vizuri.

Katika kifungu hicho, "neno la Mungu linakaa ndani yenu" (1 Yohana 2:13), UDB inaelezea wazo hili kama, "unaendelea kutii kile ambacho Mungu anaamuru." Watafsiri wengi wataona kuwa inawezekana kutumia tafsiri hii kama mwongozo.

Je, ni masuala gani muhimu katika Kitabu cha 1 Yohana?

Yafuatayo ni masuala muhimu zaidi ya maandishi katika 1 Yohana:

(See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/jit.html#translate-textvariants)

1 John 1

1 Yohana 01 Maelezo ya Jumla

Muundo na upangiliaji

Hii ni barua ambayo Yohana aliwaandikia Wakristo.

Dhana maalum katika sura hii

Wakristo na dhambi

Katika sura hii Yohana anafundisha kwamba Wakristo wote bado ni wenye dhambi. Lakini Mungu anaendelea kusamehe dhambi za Mkristo. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#forgive)

Mifano muhimu ya matamshi katika sura hii

Mifano

Katika sura hii Yohana anaandika kwamba Mungu ni mwanga. Mwanga ni mfano ya ufahamu na uadilifu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous)

Yohana pia anaandika kuhusu watu wanaotembea katika nuru au katika giza. Kutembea ni mfano ya tabia au kuishi. Watu wanaotembea katika mwanga huelewa kilicho haki na kukifanya. Watu wanaotembea katika giza hawawezi kuelewa yaliyo sawa, na wanatenda dhambi.

| >>

1 John 1:1

Sentensi Unganishi

Kitabu hiki kinaanza makusudi yake mawili - Ushirika na Furaha.

Maelezo ya Jumla

Mtume Yohana aliandika waraka huu kwa Waamini. Mifano yote ya "nyinyi" na "yenu," hujumuisha waaminio wote na yako katika wingi. Maneno "sisi" na "tu" hapa humaanisha Yohana na walie waliokuwa wameishi na Yesu. Mstari wa 1 ni nusu sentensi, unatakiwa usomwe pamoja na msitari 2. na Sentensi kamili huishia 1:3

Lile lililokuwako tangu mwanzo

Kifungu cha maneno "lile lililokuko tangu mwanzo" humaanisha Yesu, aliyekuwako kabla ya kila kitu kilichofanyika.:Tunawaandikia juu ya yule alikuwako kabla ya uumbaji wa vitu vyote

Neno la uzima

"Neno la uzima" ni Yesu Kristo. Yesu, yule anayesababisha watu waishi milele.

Uzima

Neno "uzima" mwote katika barua hii humaanisha zaidi ya uzima wa kimwili. Hapa linasimama badala ya Yesu, aliye uzima wa milele.

Na ule uzima ulifanywa kujulikana wazi

Hili linaweza kutamkwa katika mtindo tendaji. :"Mungu aulifanya uzima wa milele ujulikane kwetu" au Mungu alitufanya sisi tuweze kumjua yeye, aliye uzima wa milele"

na tumeuona

"na tumemwona yeye"

na kuushuhudia,

"na tunawatangazia na wangine kwa dhati kuhusu yeye"

uzima wa milele

"Uzima wa milele," hapa humaanisha yule ambaye hutoa uzima, Yesu. : "Yule anayetuwezesha sisi kuishi milele"

ambalo lilikuwa pamoja na Baba

"aliyekuwa na Mungu Baba"

na lilifanywa kujulikana kwetu

Huu ulikuwa ni wakati alioishi duniani. :"na alikuja kuishi miongoni mwetu"

1 John 1:3

Maelezo ya Jumla

Hapa maneno "tu...," "nasi" na "yetu" humaanisha Yohana na wale ambao wamekuwa pamoja na Yesu.

Lile ambalo tumeliona na kulisikia twalitangaza pia kwenu

Tunawaambieni pia nanyi tuliloliona na kulisikia"

muwe na ushirika pamoja nasi. Ushirika wetu ni pamoja na Baba

"muwe rafiki zetu wakaribu. Tu marafiki wa Mungu Baba"

Ushirika wetu

Hako wazi kama Yohana anawaingiza ama anawaacha wasomaji wake.

Baba...Mwana

Hivi ni vyeo muhimu vinavyoelezea uhusiano ulioko baina ya Mungu na Yesu.

ili kwamba furaha yetu iwe kamili.

"kuifanya furaha yetu ikamilike" au kutufanya sisi tufurahi kikamilifu kabisa"

1 John 1:5

Sentensi Unganishi

Tangu hapa hata sura inayoofuata, Yohana naaandika kuhusu ushirika - uhusiano wa karibu pamoja na Mungu na aamini wengine.

Maelezo ya Jumla

Hapa maneno "sisi" na "yatu.." humaanisha waaminio wote, kumlisha watu ambao Yohana alikuwa akiwaandikia. Ispokuwa imetamkwa vinginevyo, hiyo ndiyo maana kwa ukumbusho wa kitabu hiki.

Mungu ni nuru

Hii humaanisha kwamba Mungu ni safi na mtakatifu kikamilif. Zile tamaduni zinahusianisha weme na nuru zinaweza kulishika wazo hili bila ya kulifafanua fumbo lenyewe. "Mungu ni kwa uhalisia Mungu ni mwenye haki na kama nuru halisi"

ndani yake hakuna giza hata kidogo

Hii humaanisha kwamba MUngu hawezi kutenda dhambi na siyo mwovu kwa namna yo yote.Zile tamaduni zinahusianisha uovu na giza zinaweza kulielewa wazo hili bila kulielezea fumbo lenyewewe. : "Ndani yake hakuna giza la dhambi"

twatembea gizani,

Hii humaanisha "kujizoweza uovu na kutenda uovu"

damu ya Yesu Kristo,

Hii hurejelea kifo cha Yesu.

Mwanawe

Cheo hiki ni muhimu kwa Yesu, Mwana wa Mungu.

1 John 1:8

Malezo ya Jumla

Hapa neno "yeye" "lake" humaanisha Mungu.(Tazama 1:5)

hatuna dhambi

"hatutendi dhambi"

twajidanganya

"Twajilaghai wenyewe" au "tunajiambia uongo wenyewe"

kweli haimo ndani yetu

Ile kweli imezungumziwa kana kwamba lilikuwa ni jambo au kitu kambacho kingeweza kuwa ndani ya waamini.

kutusamehe dhambi zetu na kututakasa na uovu wote

Virai hivi viwili kimsingi vinamaanisha jambo lile lile. Yohana anavitumia kusisitiza kwa hakika Mungu atasamehe dhambi dhambi. : "na atazisamehe kabisa kabisa ubaya ambao tumeufanya"

twamfanya yeye kuwa muongo,

tunadai kwamba yeye ni mwongo: "ni sawasawa na kumwita yeye mwongo, kwa sababu amesema sisi sote tumetenda dhambi"

neno lake halimo ndani yetu

Kutii kuheshimu neno la Mungu kumezunguziwa kana kwamba neno lake lilikuwa ndani ya waamini. : "hatulielewi neno la Mungu wala hatutii linachokisema"

1 John 2

1 Yohana 02 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Mpinga Kristo

Katika sura hii Yohana anaandika juu ya mpinga Kristo maalum na wapinga Kristo wengi. Neno "mpinga Kristo" linamaanisha "anayepinga Kristo." Mpinga Kristo ni mtu atakayekuja siku za mwisho na kuiga kazi ya Yesu, lakini ataifanya kwa uovu. Kabla ya mtu huyu kuja, kutakuwa na watu wengi wanaofanya kazi dhidi ya Kristo; wao pia huitwa "wapinga Kristo." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#antichrist and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lastday and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#evil)

Mifano muhimu ya matamshi katika sura hii

Mfano

Kuna makundi kadhaa ya ya mifano yenye kufanana ambao yanatumiwa katika sura hii.

Kuwa ndani ya Mungu ni mfano ya kuwa na ushirika pamoja na Mungu, pia neno la Mungu na ukweli kuwa ndani ya watu ni mfano ya watu kujua na kutii neno la Mungu.

Kutembea ni mfano ya tabia, kutojua ambapo mtu anaenda ni mfano ya kutojua jinsi ya kuishi, na kujikwaa ni mfano ya dhambi.

Nuru ni mfano wa kujua na kufanya kile kilicho sahihi, na giza na upofu ni mfano ya kutojua kilicho sahihi na kutenda mabaya.

Watu wanaopotosha wengine ni mfano ya kufundisha watu mambo yasiyo ya kweli. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

<< | >>

1 John 2:1

Sentensi Unganishi

Yohana anaendelea kuandika juu ya ushirika na anaonyesha kwamba inawezekana kwa sababu Yesu yuko kati ya waaminio na Baba.

Maelezo ya Jumla

Hapa maneno "tunaye' na "zetu" humaanisha Yohana na waaminio wote. Neno "Yeye" na "zake" yaweza kumaanisha Mungu Baba au Yesu.

Watoto

Yohana alikuwa mzee na kiongozi wao. Alitumia maelezo haya kuonyesha pendo lake kwao. : "Watoto wangu wapendwa katika Kristo" au "Ninyi mliowapendwa kwangu kama watoto wangu mwanyewe"

ninawaandikia mambo haya

"Ninaandika barua hii"

Lakini kama mmoja wenu akitenda dhambi

"Lakini mmoja wenu anapotenda dhambi." Hili ni jambo ambalo inawezekana likatokea"

tunaye wakili aliye pamoja na Baba,

Neno "wakili" hapa humaanisha Yesu. : "mtu anayezungumza kwa Mungu Baba na kumsihi yeye apate kutusamehe sisi"

eye ni upatanisho kwa dhambi zetu, na siyo kwa dhambi zetu

"Aliyatoa dhabifu maisha yake mwenyewe kwa ajili yetu, na kwa sababu ya hilo Mungu husamehe dhambi zetu"

Kwa hili twajua kwamba , kama tukizishika amri zake.

"Kama tunafanya anayotuambia kufanya, kisha tutakua na uhakika kwamba tunao uhusiano na yeye"

tunamjua yeye

"tunao uhusiano na yeye"

1 John 2:4

Yeye asemaye

"Yeyote anayesema" au "mtu anayesema"

Namjua Mungu,

"Nina uhusiano mwaema na Mungu

lakini hazishiki

"hatendi" au "hatii"

amri zake

"kile mabacho Mungu anamwambia kutenda"

kweli haimo ndani yake

Kweli imezungumziwa kana kwamba ni jambo lingeweza kuwa ndani ya waaminio. : " Haamini ambacho Mungu anasema kuwa ndiyo kweli"

ashikaye

"hutenda" au "hutii"

neno lake

"kile Mungu anachombia yeye kutenda"

upendo wa Mungu

Maana zinzowezekana kuwa ni 1) "upendo wetu kwa Mungu au 2) "upendo wa Mungu kwetu."

kweli katika mtu yule upendo wa Mungu umeshakamilishwa

Hili linaweza kutamkwa kwatika muundo tendaji. : "Mungu amekamilisha pendo wa Mungu ndani ya mtu huyo," "Kwa hakika, wale wanaotii amri za Mungu ni watu wanaommpenda Mungu katika njia zote," au "upendo wa Mungu kwa watu hutimiza lengo lake wanapotenda analowaambia kutenda"

Katika hili twajua kwamba tuko ndani yake

Kirai "tuko ndani yake" humaanisha mwamini ana muuu ngano na Mungu daima au ana ushirika na Mungu unaoendelea. Katika 1Yohana, kiari/kifungu "kaa ndani yake" mara kwa mara limetumika kumaanisha kitu kile kile. : "Tunapotii analotuambia Mungu, tunaweza kuwa na uhakika kwamba tuna ushirika na yeye"

tuko ndani yake

"tuna uhusiano na Mungu"

imempasa yeye mwenyewe pia kuenenda kama vile Yesu Kristo alivyoenenda.

Unayafanya maisha ya mtu kana kwamba yalikuwa yakitembea. : "ni lazima aishi kama Yesu Kristo alivyoishi' au "inampasa pia kumtii Mungu kama tu vile Yesu Kristo alivyotii"

1 John 2:7

Sentensi Unganishi

Yohana anawapa waaminio kanuni za msingi za ushirika - utii na upendo

Wapendwa

"Ninyi watu niwapendao" au "Rafiki wapendwa"

siwaandikii ninyi amri mpya, bali amri ya zamani

"Ninaaandikia kupendana nyinyi kwa nyinyi, ambalo siyo jambo jipya kutenda bali ni amri ya zamani amabayo mmishaisikia." Yohana anamaanisha amri ya Yesu ya kupendana kila mtu na mwenzake

tangu mwanzo

Hapa, neno 'mwanzo" humaanisha wakati walipoamua kumfuata Kristo. "tangu mlipoanza kuamini katika Kristo"

Hata hivyo ninawaandikia ninyi amri mpya,

Lakini kwa namna nyingine amri ninayowaandikia ni mpya"

ambayo ni kweli katika Kristo na kwenu,

Hapa neno "Katika" humaanisha "kwa sababu ya." : "ambayo ni kweli kwa sababu ya alichotenda Kristo, na kwa sababu ya mnchotenda nyinyi"

giza linapita, na nuru ya kweli iko tayari inaangaza

"giza," hapa humaanisha uovu na "nuru" humaanisha wema. ; "kwa sababu mnaacha kutenda ovu na mna zidi kutenda jema zaidi na zaidi.

1 John 2:9

Maelezo ya Jumla

Hapa, neno "ndugu" humaanisaha Mkristo mwenza

Yeye asemeye

"Yeyote asemaye" au "Wale wanaodai." Hiaimanishi mtu yeyote.

yuko kwenye nuru

Hii ni picha ya kuishi kwa haki. Watu wanapofanya lililo haki, wanaweza kulifanya nuruni siyo kwa kificho gizani.: "hufanya lililo sahihi"

yuko katika giza hata sasa

Hii ni picha ya kuishi maisha ya dhambi. Watu wanapofanya yaliyo maovu, hupenda kujificha gizani. : "yuko gizani, akitenda lililo ovu"

hakuna jambo lolote liwezalo kumkwaza.

hakuna litakalomsababisha kujikwaa." Neno "kujikwaa" ni fumbo linalomaanisha kuanguka kiroho au kimaadili. : " hakuna litakalomsababisha kutenda dhambi" au "hatashindwa lipendezalo kwa Mungu"

yuko gizani na anatembea gizani

wazo hili linalofanana limesemwa mara mbiili kusisitiza kulivyo uovu kumchukia mwamini mwenzako. "anaishi gizani au anaishi katika giza la dhamb

hajui wapi aendako

Hii ni picha ya Mwamini anayeishi isivyompasa Mkristo kuishi. : "hata hajui kwamba analofanya ni ovu"

giza limeyapofusha macho yake

"giza limemfanya asiweze kuonona." giza ni fumbo au mfano kwa ajili ya dhambi au uovu. : "dhambi imefanya isiwezekane kwake kuielewa kweli"

1 John 2:12

Maelezo ya Jumla

Yohana anaelezea sababu inayomfanya kuandika barua yake ama kwa vikundi vyenye umri mbalimbali au kwa waamini wanaotofautiana katika ukomavu. Barua yenyewe imeandikwa kwa mtindo wa kishairi.

watoto wapendwa

Yohana ni mzee na kiongozi wao. Alitumia maelezo haya kuonyesha upendo kwa aji yao. : "Watoto wangu wapendwa katika Kristo" au "ninyi mlio wapendwa kama watoto wangu mwenyewe." Tazama maelezo katika sura ya 2:1 uone linavyofafanuliwa.

dhambi zenu zimesamehewa

"Mungu husamehe dhambi zenu"

kwa ajili ya jina lake.

"jina lake" humaanisha Kristo na alivyo yeye. :"kwa sababu ya kile Kristo amefanya kwa ajili yenu"

Nawaandikia ninyi, akina baba,

Neno "akina baba" hapa linaweza kuwa fumbo au mfano ukimaanisha waamini waliokomaa. : "Ninawaandikia ninyi, waamini mlikoamaa

mnamjua

"mna uhusiano na"

yeye aliye wa tangu mwanzo.

"yeye ambaye amekuwa akiishi siku zote" au "yeye ambaye amekuwako siku zote." humaanisha Yesu au Mungu Baba."

vijana,

Hili inawezekana kumaanisha wale wasio waamini wapya tena, bali ni wale wanokua katika ukomavu wa kiroho

mko imara,

Hapa neno "imara" halimaanishi nguvu za kimwili za waamini, bali ni ule uaminifu wao kwa Kristo.

neno la Mungu linakaa ndani yenu

Mwandishi anamaanisha lile ongozeko la uaminifu wa waaminio kwa Kristo na ufahamu wao juu Yake kana kwamba alikuwa akiongelea neno la Mungu likiishi ndani yao. : "Ninyi mnaolijua neno la Mungu"

mmemshinda

Mwandishi anazungumzia juu ya maaminio kukataa kumfuata Shetani na kuipinga kwao mipango yake kana kwamba mambo hayo yamekuwa ni jambo la kumshinda yeye.

1 John 2:15

Msiipende dunia

Neno "dunia" katika 2:15-17 humaaniha mabo yote watu hutaka kufanya , mambo ambayo hayamtukuzi Mungu. : "Msienende kama watu wa duniani wasiomheshimu Mungu"

wala mambo yaliyo katika dunia

"msitake mambo yale yale wanayoyataka wale wasiomheshimu Mungu"

Kama kuna yeyote ambaye huipenda dunia, upendo wa Baba haumo ndani yake.

Mtu hawezi kuipenda dunia hii pamoja na wale wote wasiomheshimu Mungu na kumpenda Baba wakati huo huo.

upendo wa Baba haumo ndani yake

"hawa hamendi Baba"

tamaa ya mwili, tamaa ya macho, na kiburi cha uzima-

Hii ni orodha ya baadhi ya mambo yaliyomo duniani. Nayo huelezea inamaana nini kusema "kila kilichomo dunianai"

tamaa ya mwili

"tamaa kali ya kuwa starehe ovu za kimwili"

tamaa ya macho,

"tamaa kali ya kuwa na vitu tuvionavyo"

kiburi cha uzima

"Kiburi cha uzima." hili laweza kuashiria pande zote mali na nia. "kujivunia alicho nacho mtu au anachotenda" au "kiburi ambacho watu husikia kwa sababu ya vitu vyao na kile mtu amefanya."

uzima

Hili lingeweza kumaanisha vitu walivyo navyo watu ili kuishi, vitu kama vile mali, utajiri pamoja na nia.

hayatokani na Baba

"hayatoki kwa Baba" au "sivyo hivyo Baba alivyotufundisha kuishi"

yapita

"yanapita" au "siku moja hayatakuwepo"

1 John 2:18

Sentensi Unganishi

Yohana anaonya juu ya wale waliokinyume na Kristo

Watoto wadogo

"Wakristo wasiokomaa." Tazama sura 2:1 uone lilivyofafanuliwa

ni wakati wa mwisho

Kile kirai "Wakati wa mwisho" humaanisha muda kabla ya kurudi kwa Yesu. "Karibu Yesu atarudi"

wapingakristo wengi wamekuja,

"kuna watu wengi waliokunyume cha Kristo"

kwa hali hii tunajua

"na kwa sababu ya hili tunajua" au "na kwa sababu wapngakristo wametokea, tunajua"

Walikwenda zao wakatoka kwetu

"walituacha"

kwa kuwa hawakuwa wa kwetu.

"lakini kwa kweli hawakuwa wa kwetu kwa namna yoyote" au "kwa uhalisia hawakuwa sehemu ya kundi letu katika nafasi ya kwanza ." Sababu iliyofanya waondoke ni kwamba, kwa kweli sehemu ya kundi; yaani hawakuwa waaminio katika Yesu Kristo.

Kama wangekuwa wa kwetu wangeendelea kuwa pamoja nasi

"Tunajua hivi kwa sababu wasingekuwa wametuacha kama kwa kweli wangelikuwa waamini.

1 John 2:20

Maelezo ya Julama

Katika Agano La Kale neno kutia "mafuta" lilimaanisha kumimina mafuta juu ya mtu ili kumtenga kwa ajili ya kumtumikia Mungu.

Lakini mumetiwa mafuta na yule Mtakatifu

"Bali Yule Mtakatifu amewatia mafuta ninyi. Hapa "kutia mafuta" humaanisha kazi ya Yesu kuwapa waaminio Roho Mtakatifu ili kuwatenga kwa ajili ya kumtumikia Mungu. : "Lakini Kristo, aliye Mtakatifu, amwapa ninyi Roho wake Mtakaifu"

hakuna uongo kwa ile kweli

Hapa tendo la kuema uongo limzungumzwa kana kwamba ni kitu. : "hakuna uongo ujao kutoka kwa Mungu ambaye ni kweli.

1 John 2:22

Nani ni mwongo bali ni yeye anayepinga kwamba Yesu ni Kristo? Huyu mtu ni mpinga kristo

Nani ni mwongo? ni yeyote akanaye ukweli kwamba Yesu ni Kristo." Yohana alitumia swali kusisitiza waongo ni nani.

anayemkana Baba na Mwana.

"hukataa kusema kweli kuhusu Baba na Mwana" au "humkataa Baba na Mwana."

Baba... Mwana

Hivi ni vyeo muhimu ambavyo huelezea uhusiano kati ya Mungu na Yesu.

ana Baba

"ni wa Baba"

amkiriye Mwana

Husema kweli kuhusu Mwana"

ana Baba

"ni wa Baba"

1 John 2:24

Sentensi Unganishi

Yohana anawakumbusha waamini kuendelea katika lile walilokisikia hapo kwanza

Maelezo ya Jumla

Hapa neno "ninyi" ni katika wingi nna humaanisha watu ambao Yohana anawaandikia pia na waamin wote.

kile mlilosikia toka mwanzo acha liendelee kuwa ndani yenu.

"Kumbukeni na kuamini lile mlilolisikia tangu mwanzo>" Walilisikiaje, walilolisikia, na mwamwazo humaanisha nini, linaweza kuwekwa wazi. "endeleeni kutumaini tulilowafundisha kuhusu Yesu kama tu vile ambavyo mmetumaini tangu mwe waamini.

Lile mlilolisikia tangu mwanzo

"tulilowafundisha kuhusu Yesu mlipoanza kuwa kuwa waamini"

ikiwa mlilolisikia hukaa ndani yenu

Neno "hukaa" linazungumzia kuhusu uhusiano, siyo wakovu. "ikiwa mtaendelea kutumaini tullowafundisha hapo kwanza"

pia mtakaa ndani ya Mwana na Baba

"pia mwe na uhusiano pamoja na Mwana pamoja na Baba." Tazama maelezo katika 2:4 Uone lilivyofafanuliwa

Na hii ni ahadi aliyotupatia sisi: uzima wa milele.

"na hivi ndivyo alivyotuahidi sisi kutupa - uzima wa milele" au " Na ametusababisha kuishi milele.

uzima

Neno "uzima" katika barua nzima humaanisha zaidi ya uzima wa kimwili. Tazama maelezo katika 1:1 uone lilivyofafanuliwa

wangeliwakosesha

"wanaotaka kuwaondoa njiani." Kuna wale ambao wangejaribu kuwaondoeni kwa Mungu na kweli Yake" "wangewasababisha kuamini uongo"

kosesha

Shawishi mtu kutomtii Mungu limezugumziwa kana kwamba linlikuwa likimtoa mtu kwanya njia sahihi ya kufuata

1 John 2:27

Sentensi Unganishi

Kuazia mstari 29, Yohana anatambulisha wazo la kuzaliwa kwenye familia ya Mungu. Mistari inayotangulia inaonyesha kwamba waaminio huendelea kutenda dhambi, sehamu hii inaonyesha waamini pia wana asili mpya ambayo haitendi dhambi. Inaendelea kuelezea kwamba wanaweza kutambuana kila moja.

Na kwa ajili yenu

Kifungu hiki kinamwonyesha Yohana akiwaambia pia ilivyowapasa kuishi kama wafuasi wa Yesu badala ya kuwafuata wale waliokinyume na Kristo.

yale mafuta

Humaanisha "Roho wa Mungu." Tazama maelezo katika 2:20 uone linavyofafanuliwa

mambo yote

Kirai hiki ni baalagha ambayo hutia chumvi mambo au matukio. : "kila kitu mnachohitaji kukijua"

kaeni ndani yake.

"ishini kwa ajili ajili yake." Tazama uone jinsi kurai hiki kilivyotafsiriwa katika 2:4. Jinsi mtu anavyokaa humaanisha ushirika au uhusiano wake.

Na sasa

Kirai hiki kimetumika kuunda sehemu mpya ya barua.

watoto wapendwa

Yohana alikuwa mtu mzeena kiongozi wao. Alitumia maelezo haya kuonyesha pendo lake kwao. : "watoto wangu wapendwa katika Kristo" au "ninyi mlio kama wapendwa kwangu kama wato wangu mwenyewe. Tazama ufafanuzi wake katika 2:1

atakapotokea,

"tutamwona yeye"

ujasiri

"kujiamini"

wakati atakapotokea

"atakapokuja tena"

amezaliwa na yeye.

amekuwa mzaliwa wa Mungu" au ni mtoto wa Mungu"

1 John 3

1 Yohana 03 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Watoto wa Mungu

Mungu aliumba watu wote, lakini watu wanaweza tu kuwa watoto wa Mungu kwa kumwamini Yesu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#believe)

Kaini

Kaini alikuwa mwana wa mtu wa kwanza, Adamu, na mwanamke wa kwanza, Hawa. Alimwonea wivu ndugu yake na kumwua. Wasomaji hawawezi kujua Kaini ni nani ikiwa hawajasoma kitabo cha Mwanzo. Wanaweza kusaidiwa ikiwa unawaelezea hivi.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

"Kujua"

Kujua" ni neno la kitenzi kinachotumika kwa njia mbili tofauti katika sura hii. Wakati mwingine hutumiwa kuhusu kujua ukweli, kama katika 3:2, 3:5, na 3:19. Wakati mwingine inamaanisha uzoefu na kuelewa mtu au kitu, kama katika 3:1, 3:6, 3:16, na 3:20. Lugha zingine zina maneno tofauti kwa maana hizi tofauti.

"Yeye anayezingatia amri za Mungu anakaa ndani yake, na Mungu anakaa ndani yake"

Wasomi wengi wanaamini kama hii inamaanisha kubaki katika mapenzi ya Mungu wala sio kumaanisha kuokolewa. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#eternity and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#save)

<< | >>

1 John 3:1

Angalia ni pendo la namna gani ametupatia Baba.

"Fikiria kuhusu kiasi gani Baba yetu anavyotupenda sisi."

Sisi...Tu.

Katika 3:1-3 viwakilishi nomino hivi, humtaja Yohana, wasikilizaji wake, na waumini wote.

Lazima tuitwe watoto wa Mungu.

Hii inaweza kutafsiriwa kwa kitenzi tendaji: "Baba lazima atuite sisi watoto wake."

Watoto.

Hapa hii inamaanisha watu wa Mungu kwa imani katika Yesu.

Ulimwengu haututambui, kwa sababu hakumtambua Yeye.

Hapa "ulimwengu" humaanisha watu ambao hawamheshimu Mungu. Kile ambacho ulimwengu haukijui, hakiwezi kufanywa dhahili: Wale ambao hawamheshimu Mungu, hawajui kwamba sisi ni wa Mungu, kwa sababu hawakumjua Mungu.

Haijadhihirika bado.

Hii inaweza kutafsiriwa kwa kitenzi tendaji: "Mungu hajadhihirisha."

Na kila mtu ambaye ana ujasiri huu kuhusu wakati ujao ulioelekezwa kwake, hujitakasa mwenyewe kama yeye alivyo mtakatifu.

"Kila mtu ambaye anatarajia kwa ujasiri kumuona Kristo kama alivyo, ataendelea kujitakasa mwenyewe kwa sababu Kristo ni mtakatifu."

1 John 3:4

Anafanya uasi.

"Ana kataa kutii sheria ya Mungu"

Ninyi.

Hapa neno "Ninyi" ni wingi na inawalenga watu ambao Yohana anawaandikia.

Kristo alidhihirishwa.

Hii inaweza kutafsiriwa kwa kitenzi tendaji: "Kristo alitokea" au "Baba alimfunua Kristo."

Kudumu katika yeye.

"Ni kuendelea kufanya anayotaka Yesu."

Hakuna ambaye...amemuona au amemfahamu.

Yohana hutumia neno "amemuona" na "amemfahamu" kusisitiza kwamba mtu ambaye hudumu katika kutenda dhambi hajawahi kukutana na Yesu katika maana ya kiroho. "Hakuna ambaye...hajawahi kabisa kumwamini Yeye."

1 John 3:7

Watoto wapendwa.

Watoto wanaopendwa/waumini wanaopatana naye.

Msiruhusu mtu yeyote kuwapotosha.

"Msikubali mtu yeyote awafanye wajinga" au "msikubali mtu yeyote awadanganye."

Atendaye haki ni mwenye haki, kama Kristo alivyo mwenye haki.

"Anayetenda kilicho sahihi anampendeza Mungu kama Kristo anavyompendeza Mungu."

Hutenda dhambi.

"Huendelea kutenda dhambi"

Ni ya Ibilisi.

"Humilikiwa na shetani au ni kama shetani"

Kutoka mwanzo.

Hii inalenga hasa nyakati za uumbaji kabla ya binadamu hawajaanguka dhambini. "Tangu nyakati za mwanzo za uumbaji."

Mwana wa Mungu alidhihirishwa.

Hii inaweza kutafsiriwa kwa fungu la maneno yanayoonesha kitendo: "Mungu alimudhihirisha Mwanawe."

Mwana wa Mungu.

Hili ni jina mhimu kwa Yesu ambalo hufafanua uhusiano kwa Mungu.

1 John 3:9

Yeyote aliyezaliwa na Mungu.

Hii inaweza kutafsiriwa kwa fungu la maneno lenye kitendo: "Yeyote ambaye Mungu amemfanya kuwa mwana wake."

Hafanyi dhambi.

"Hawezi kuendelea kutenda dhambi."

Mbegu ya Mungu.

Hii inalinganisha mbegu ya kawaida inayo pandwa katika udongo na hustawi kwa uwezo wa Roho Mtakatifu ambaye Mungu humweka ndani ya waumini, Roho huwapa nguvu za kupinga dhambi na kufanya kile kinachomfurahisha Mungu. Hii ingeweza kutafsiriwa kama hivi: "Roho Mtakatifu"

Amezaliwa na Mungu.

Hii inaweza kutafsiriwa kama fungu la maneno yenye kitendo: "Mungu amempa maisha mapya ya kiroho" au "Ni mtoto wa Mungu."

Kwa jinsi hii watoto wa Mungu na watoto wa shetani wanajulikana.

Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi yenye kuonesha tendo: "Hivi ndivyo tunavyowajua watoto wa Mungu na watoto wa shetani."

Yeyote asiye fanya mambo ya haki huyo si wa Mungu, wala ambaye hampendi ndugu yake.

Hapa "ndugu" humaanisha Wakristo wapendwa. Wale tu wanaofanya haki ndio wa Mungu, na wale tu ambao huwapenda ndugu zao."

1 John 3:11

Tuna pasa kupenda.

Hapa, neno "tuna" linalenga waumimini wote.

Ndugu.

Katika tukio hili, neno ndugu linamaanisha mdogo wake na Kaini, Abeli.

Na kwa nini alimuua?Kaw sababu

Yohana anatumia swali kuwafundisha wasikilizaji wake. Hii ingeweza kutafsiriwa kama usemi: "Alimuua kwa sababu."

Kazi zake zilikuwa na uovu, na kazi za ndugu yake zilikuwa za haki.

"Kwa sababu daima alifanya mambo maovu na ndugu yake alikuwa akifanya mambo mazuri."

1 John 3:13

ndugu

"Waamini wenzangu."

Kama ulimwengu utawachukia

Hapa neno "ulimwengu" lina maana ya watu ambao hawamheshimu Mungu. "Kama hao wasiomheshimu Mungu watawachukia.

Tumetoka katika mauti kuingia uzimani.

"Hatuko tena wafu kiroho bali tu wazima kiroho."

Kudumu katika mauti.

"Ni kuendelea kufa kiroho."

Yeyote anaye mchukia ndugu yake ni muuaji.

Hii ni kumlinganisha mtu anaye mchukia muumini mwingine na muuaji. Kwa kuwa chuki ni chanzo cha mauaji, Mungu humuwazia mtu yeyote mwenye chuki kuwa mwenye hatia kama aliye muua mtu. "Yeyote anayemchukia muumini mwenzake ana hatia kama muuaji."

Uzima wa milele haukai ndani ya muuaji.

"Uzima wa milele" ni uhai ambao Mungu hutupatia waumini baada ya kufa, lakini pia ni nguvu ambayo Mungu huwapatia waumini katika uzima huu, kuwasaidia waache kufanya dhambi na wafanye yale yanayo mpendeza yeye. "Muuaji hana nguvu za uzima wa kiroho zinazofanya kazi ndani yake."

1 John 3:16

Kristo aliutoa uhai wake kwa ajili yetu.

Maelezo haya humaanisha: "Kristo kwa kupenda kwake mwenyewe aliutoa uhai wake kwa ajili yetu" au "Kristo kwa kupenda kwake alitufia sisi."

Mali za ulimwengu.

"Mali zinazomilikiwa kama vile pesa, chakula, au nguo."

Humuona ndugu yake mwenye uhitaji.

"Na humtambua muumini mwenzake anayehitaji msaada."

Na huufunga moyo wake wa huruma kwa ajili yake.

Maelezo haya humaanisha kwamba, "lakini hamwonei huruma." au lakini hapendi kumsaidia."

Upendo wa Mungu unakaaje ndani ya mtu huyo?

Yohana anatumia swali kuwafundisha wasikilizaji wake. Hii ingeweza kutafsiriwa kama usemi: "Upendo wa Mungu haumo ndani yake."

Watoto wangu wapendwa.

"Watoto au wapendwa waumini wenzi wangu."

Haya tusipende kwa maneno wala kwa mdomo.

Kifungu hiki, "kwa maneno" na "kwa mdomo" yote mawili yanalenga kile ambacho mtu anasema. " Usiseme tu ili mradi kwamba unawapenda watu."

Bali katika matendo na kweli

"Bali onesha kwamba kweli unawapenda watu kwa kuwasaidia."

1 John 3:19

Sentensi Unganishi

Hapa huenda Yohana anamaanisha kwamba uwezo wa waminiowa kumpenda Mungu na kupenda wao kwa wao kwa thati (tazama mstari wa 18) ni in ishara kwamba maisha yao mapya hasa asili yake ni ukweli kuhusu Kristo.

Sisi tunatokana na kweli.

"sisi ni wa hiyo kweli" au :"tunaishi kufuatana na jinsi Yesu alivyotufundisha."

mioyo yetu inathibitika

neno "moyo" humaanisha hisia. "hatutahisi hatia."

Ikiwa mioyo yetu yatuhukumu

Hii ni methali au fumbo. : "kama tuajua kwamba tumefanya dhambi na matokeo yake tunasikia hatia"

Mungu ni mkuu kuliko mioyo yetu.

"Mungu hujua zaidi ya mtu na huhukumu vyema" Athari za ukweli huu labda huenda ni kwamba Mungu ni mwenye rehema zaidi ya dhamiri zetu ambavyo zingesema. Ubora huu wa Mungu umeelezewa kwa neno "mkuu." Mungu hujua zaidi ya tunavyojua.

Wapendwa

"Ninyi watu ninaowapenda" au "rafiki wapendwa." Tazama lilivyotafriwa katika 2:7

na tunafanya mambo yanayopendeza mbele zake.

Maoni ya Mungu yameongelewa kana kwamba yanategemea anayoona yakitokea mbele zake. "na hufanya linalompendeza yeye"

1 John 3:23

Hii ndio amri yake.

"Hiki ndicho ambacho Mungu anataka tufanye."

Mwana

Hili ndilo Jina Mashuhuri la Yesu, Mwana wa Mungu.

Dumuni ndani yake, na Mungu hudumu ndani yake.

Daima kuwa na ushirika endelevu na Mungu.

1 John 4

1 Yohana 04 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Roho

Neno hili "roho" linatumiwa kwa njia tofauti katika sura hii. Wakati mwingine neno "roho" linamaanisha viumbe wa kiroho. Wakati mwingine inahusu tabia ya kitu fulani. Kwa mfano "roho ya mpinga Kristo," "roho ya kweli," na "roho ya hitilafu" inamaanisha kile ambacho ni mfano wa mpinga Kristo, ukweli, na kosa. "Roho" (iliyoandikwa na herufi kubwa "R") na "Roho wa Mungu" inamaanisha Mungu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#antichrist)

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Kupenda Mungu

Ikiwa watu wanampenda Mungu, wanapaswa kuonyesha katika njia wanayoishi na jinsi wanavyowatendea watu wengine. Kufanya hivyo kunaweza kutuhakikishia kuwa Mungu ametuokoa na kwamba sisi ni wake, lakini kupenda wengine haituokoi. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#save)

<< | >>

1 John 4:1

Maelezo ya Jumla

Yohana anatoa onyo dhidi ya walimu wa uongo ambao hufundisha kinyume cha Kristo kuwa na mwili wa kibinadamu na waalimu huongelea kama wale wanaopenda mazungumzo ya ulimwengu

Wapendwa

"Nyinyi watu ninaowapenda" au "Rafiki wapendwa." Tazama linavyofafanuliwa 2:7

msiiamini kila roho

Hapa, neno "roho" humaanisha uwezo au nguvu zakiroho au nafsi inayompa mtu ujumbe au unabii. "msimtumaini kila nabii anayedai kuwa anao ujumbe kutoka kwa roho"

zijaribuni roho

Hapa, neno "roho" humaanisha uwezo au nguvu zakiroho au nafsi inayompa mtu ujumbe au unabii. : "hakikisheni kwamba mnasikiliza kwa makini kwa anayoyasema nabii"

jaribu

"thibitisha"

kila roho itakayokiri kuwa Yesu Kristo amekuja katika mwili

"amechukua umbo la mwili" au amekuja katika mwili unoonekana"

Hii ni roho ya mpinga kristo

"wao ni walimu wanaliokinyume na Kristo" au "wao ni walimu wanaompinga Kristo"

mpinga kristo, ambayo mliyoisikia kuwa inakuja

"mpingakristo. Mmekwisha kusikia kwamba watu kama hao wanakuja miongoni mwetu"

inakuja, na sasa tayari iko duniani.

"wanakuja. Na hata sasa tayari wako hapa"

1 John 4:4

watoto wapendwa

Yohana alikuwa mzee tena kiongozi wao. Alitumia maelezo haya kuonyesha pendo lake kwao. "watoto wangu wapendwa katika Kristo" au "ninyi mlio kama watoto wangu mwenyewe ninaowapenda." Tazama 2:1lilivyofafanuliwa

mmekwisha washinda

"hamjawaamini waalimu wa uongo"

yeye aliye ndani yenu

"Mungu aliyemo ndani yenu"

yeye aliye katika ulimwengu

Uwezekano wa maana mbili ni 1) "wale waalimu wa kidunia" au 2) "Shetani aliyeko ulimwenguni

ulimwengu

Jina "ulimwengu" humaanisha watu wot wasiomtii Mungu pia humaanisha mfumo uovu ukaao katika ulimwengu wa dhambi

Wao ni wa ulimwengu,

"Wale waalimu wa uongo ni watu wasiomtii Mungu"

kwa hiyo wanachokisema ni cha ulimwengu,

"kwa hiyo hufundisha mawazo yaliyokinye na Mungu"

na ulimwengu huwasikiliza wao.

kwa hiyo watu wasiomtii Mungu huwasikiliza wao"

1 John 4:7

Maelezo ya Jumla

Yohana anaendelea kufundisha kuhusu asili mpya. Anawafundisha wasomaji wake juu ya pendo lamungu na kupendana wao kwa wao

Wapendwa

"Nyinyi watu ambao ninawapenda" au "Rafiki wapendwa" Tazama lilifasiriwa katika 2:7

tupendane sisi kwa si

"waaminio ni lazima wapendane wao kwa wao"

na kila mmoja apendaye amezaliwa na Mungu na kumjua Mungu.

"kwa sababu wale wanaowapenda waamini wenzao wamefanyika watoto wa Mungu na humjua yeye"

kwa sababu pendo latoka kwa Mungu.

"kwa sababu Mungu hutusababisha kupendana sisi kwa sisi"

amezaliwa na Mungu

Hii ni methali au fumbo ambalo humaanisha mtu mtu fulani kuwa na uhusiano na Mungu kama mtoto kwa babaye.

Yeye asiyependa hamjui Mungu, kwa sababu Mungu ni upendo.

"Asili ya Mungu ni kupena watu. Wale wasiowapenda waamini wenzao hawamjui Mungu kwa sababu tabia ya Mungu ni kupenda watu.

Mungu ni upendo

Hii ni mithali au fumbo linalomaanisha "tabia ya Mungu ni upendo"

1 John 4:9

Katika hili pendo la Mungu lilifunuliwa miongoni mwetu,

"Kwa hili Mungu alionyesha kwamba alitupenda"

pendo la Mungu lilifunuliwa

Ule uhalisa kwamba Mungu anampenda kila mtu yamengumzwa kana kwamba yalikuwa kitu ambacho kwacho Mungu angeweza kwao.

ili tungeishi kwa sababu ya yeye

"kutuwezesha kuishi miliele kwa sababu ya kile Yesu alifanya

Katika hili pendo

Mungu alituonyesha sisi hasa pendo ni nini

pendo, si kwamba tulimpenda Mungu, lakini yeye alitupenda, na

"pendo: pendo la kweli siyo namna tuvyompenda Mungu, bali ni jinsi alivyotupenda sisi, na"

akamtuma Mwanawe awe fidia ya dhambi zetu.

Hapa "fidia" hurejelea tukio la ambalo kwalo Mwana alifanyika dhabihu kwa ajili ya dhambi kwa ajili ya dhambi za watu wote. : "An alimtuma Mwanawe kutoa mwenyewe kuwa dhabihu ili kwamba Mungu angeweza kutusamehe dhambi zetu

1 John 4:11

Wapendwa

"Enyi watu niwapendao," au "rafiki wapendwa." Tazama 2:7

ikiwa Mungu alitupenda sisi

"kwa kuwa Mungu alitupenda sisi katika njia hii"

kupendana sisi kwa sisi

Waaminio wanapaswa kuwapenda waamini wengine.

Mungu anakaa ndani yetu... tunakaa ndani yake

"Mungu anao uhusiano nasi... tunao uhusianao na Mungu naye ana uhusiano nasi." Tazama lilivyotafsiriwa 2:4

kwa sababu ametupa

"kwa sababu alitupatia Roho wake" au "amekwisha mweheka roho wake nadani yetu," hata hivyo, kirai hiki hakiashirii Mungu ana kiasi kidogo cha Roho Wake alichobaki nacho baada ya kuwa ametupatia sisi sehemu yake.

Na tumeona na kushuhudia kuwa Baba amemtuma Mwana kuwa mwokozi wa ulimwengu.Roho wake.

"Nasi mitume tumewona MWana wa Mungu na tunamwambia kila mtu kwamba Mungu, Baba, amemtuma MWana ili kuokoa watu hapa duniani"

Baba...Mwana

Hivi ni vyeo muhimi ambavyo huelezea uhusiano kaika ya Mungu na Yesu.

1 John 4:15

Kila anayekiri kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu

"Wale wanaousema ukweli kuhusu, kwamba yeye ni Mwana wa Mungu"

Mwana wa Mungu

Hiki ni cheo muhimu kwa ajili ya Yesu kinachoelezea uhusiano wake kwa Mungu.

hukaa ndani yake

"Mungu anauhusiano naye na yeye pia anauhusianao na Mungu. Tazama 2:4

Mungu ni Pendo

Hii ni mithali ambaoy humaanisha kuwa "tabia ya Mungu ni upendo." Tanzama 4:7

na yeye anayekaa ndani ya upendo anakaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake.

"wale wanaoendelea kupenda wengine wanao uhusianao wa karibu na Mungu, naye Mungu anao uhusiano wa karibu nao"

1 John 4:17

Kwa sababu hii, pendo hili limekwisha kamilishwa miongoni mwetu, ili tuwe na ujasiri

Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. (Maana zinazowezekana ni 1) " Kwa sababu kwa sababu hii" hurejea 4:14 : "Kwababu yeyote akaaye katika pendo hukaa ndani ya Mungu na Mungu ndani yake, Mungu amelifanya pendo lake kamili kwa ajili yetu, na kwa hiyo tunaweza kuwa na ujasiri kamili" au 2) "Kwa sababu hii" hurejea kwa "tuwe na ujasiri." : "Tuna ujasiri kwamba Mungu atatupokea katika siku anayohukumu kila mmoja, kwa hiyo tunajua amelifanya pendo lake kuwa kamili"

pendo hili limefanywa timilifu miongoni mwetu

"hivi ndivyo ambavyo Mungu amelifanya pendo lake kuwa kamili kwa ajili yetu"

kwa sababu kama yeye alivyo, na sisi ndivyo tulivyo katika ulimwenngu huu

"kwa sababu uhusiano alionao Yesu pamoja na Mungu ni uhusiano ule ule tulionao sisi pamoja na Mungu ulimwenguni humu"

pendo kamili huitupa hofu nje

Hapa "pendo" limeelezwa kama nafsi yenye uwezo wa kuondoa hofu. Pendo la Mungu ni kamilifu, haitupasi kuogopa"

kwa sababu hofu huhusiana na hukumu

"kwa sababu tunaogopa kama tunafikiri kwamba Mungu atakapokuja atatuadhibu kila mmoja"

Lakini yeye aogopaye hajakamilishwa katika pendo.

"Mtu anapoogopa kwamba Mungu atamwdhibu yeye, inamaanisha kwamba pendo lake si kamili"

1 John 4:19

1Yohana 4:19-21

Sisi amchukiaye ndugu yake yeyote asiyempenda ndugu yake anayemuona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hajamuona amri tuliyo nayo kutoka kwake

1 John 5

1 Yohana 05 Maelezo ya Jumla

Dhana maalum katika sura hii

Watoto waliozaliwa kutoka kwa Mungu

Watu wanapoamini Yesu, Mungu huwafanya watoto wake na kuwapa uzima wa milele. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#believe)

Kuishi Kikristo

Watu wanaomwamini Yesu wanapaswa kutii amri za Mungu na kupenda watoto wake.

Changamoto nyingine za kutafsiri katika sura hii

Kifo

Wakati Yohana anaandika juu ya kifo katika sura hii, anaelezea kifo cha kimwili. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#death)

"Ulimwengu wote upo katika uwezo wa mwovu"

Maneno "yule mwovu" yanamaanisha Shetani. Mungu amemruhusu aongoze ulimwengu, lakini hatimaye Mungu ana mamlaka juu ya kila kitu. Mungu anawaweka watoto wake salama mbali na mwovu. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#satan)

__<< | __

1 John 5:1

Maelezo ya Jumla

Yohana anaendelea kuwafundisha wasomaji wake kuhusu upendo wa Mungu na upedo ambao waaminio wanapaswa kuwa nao kwa sababu mekuwa na hali hii mpya kutoka kwa Mungu

amezaliwa na Mungu

"ni mwana wa Mungu"

Kwa hili twajua kwamba twawapenda watoto wa Mungu: tunapompenda Mungu na kutekeleza amri zake.

"Tunapompenda Mungu na kutenda atuamruyo, ndipo tunatambua kwamba tunawapenda watoto wake"

Hivi ndivyo tunavyompenda Mungu kwamba twazishika amri zake.

"Kwa sababu tunapofanya atuamruyo, hilo ndilo pendo la Mungu"

Na amri zake ni nyepesi.

"Na anayotuamru siyo gumu"

nzito

"lenye kuponda," "lenye kukandamiza" au "gumu"

1 John 5:4

kila aliyezaliwa na Mungu

"watoto wote wa Mungu"

huushinda ulimwengu

"wanaushindi juu ya ulimwengu," "hufaulu dhidi ya ulimwengu," au "hukataa kufanya mambo maovu wayafanyayo wasioamini"

Na huu ndio ushindi wa kuushinda ulimwengu: imani yetu

"Imani yetu hupatia nguvu ya kuzuia lolote ambalo lingetutia katika ktenda dhambi dhidi ya Mungu"

Ni nani anayeushinda ulimwengu?

Yohana alitumia swali hili kutambulisha jambo fulani alilotaka kufundisha. "Nitaambia anayeshinda ulimwengu"

ulimwengu

ujumbe huu "ulimwengu? kwa kumaanisha watu wote wenye dhambi na mfumo mwovu wa ulimwengu"

Ni yule aaminiye kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu.

Hili halimaanishi mtu maalum bali kwa yeyote anayeamini kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu.

Mwana wa Mungu

hiki ni cheo muhimu kwa Yesu kinachoelezea uhusiano wake kwa Mungu

1 John 5:6

Sentensi Unganishi

Yohana anafundisha kuhusu Yesu Kristo na aliyosema Mungu kuhusu yeye.

Huyu ndiye aliyekuja kwa maji na damu- Yesu Kristo

"Yesu Kristo ndiye aliyekuja kwa maji na damu. hapa "maji" ni taashira au mfano labda huenda kwa ajili ya ubatizo wa Yesu, na "damu" husimama kwa niaba ya kifo cha Yesu msalabani. : "Mungu alionyesha kwamba Yesu Kristo ni Mwanawe kwenye ubatizo wa Yesu na kifo chake masalabani"

Hakuja tu kwa maji bali kwa maji na damu

Maji humaanisha ubatizo wa Yesu na damu humaanisha kifo cha Yesu msalabani. : "Mungu hakutuonyesha sisi kuwa Yesu alikuwa Mwanawe kupitia ubatizo wake tu, bali pia kwa njia ya kifo chake msalabani"

1 John 5:9

Kama tunaupokea ushuhuda wa wanadamu ushuhuda wa Mungu ni mkuu

"Kama tunaamini wasemayo watu, basi ni lazima tuamini asemacho Mungu kwa sababu Yeye daima huisema kweli"

tunaupokea ushuhuda wa wanadamu

uhalisia kwamba watu huutoa ushahidi au kushuhudia juu ya mambo mbalimbalia limezungumziwa hapa kana kwamba ni kitu amabacho wengine hukipokea.

ushuhuda wa Mungu ni mkuu

usuhuda wa Mungu ni mkuu na muhimu na wa kutegemewa zaidi

amwaminiye Mwana wa Mungu ana ushuhuda ndani yake m

mtu yeyote anayemwamini Yesu hujua kuwa hakika Yesu ni Mwana wa Mungu"

amemfanya yeye kuwa mwongo,

"anamwita Mungu mwongo"

kwa kuwa hakuuamini ushuhuda ambao Mungu ameuleta kuhusu Mwanawe.

"kwa sababu haamini kwamba Mungu aliseama kweli kuhusu Mwanawe"

1 John 5:11

Na ushuhuda ndio huu

"Hivi ndivyo Mungu anavyosema"

uzima

Hapa "uzima" husimama badala ya haki ya kuishi milele kwa neema na upendo wa Mungu. Tazama 1:1

uzima huu umo ndani ya Mwanawe.

uzima huu ni kwa njia ya Mwanawe, "Tutaishi milele kama tutaungana na Mwanawe" au "tutaishi milele kama tutakuwa na muungano na Mwanawe"

Mwana

Hiki ni cheo muhimu kwa Yesu, Mwana wa Mungu.

Aliye naye Mwana ana uzima

Kuwa katika uhusiano wa karibu na Yesu kunazungumzia ni kama kuwa na Mwana. "Yeye aaminiye katka Mwana wa Mungu anao uzima wa milele"

1 John 5:13

Maaelezo ya Jumla

Hii inaanzisha mwisho wa barua ya Yohana. Anawaambia wasomaji wakke kusudi lake la mwisho kwa barua yake na anawapa mafundisho kadha ya mwaisho.

mambo haya

"barua hii"

ninyi mnaoamini katika jina la Mwana wa Mungu

Hapa "jina" ni Taashira au Ishara inayomwakilisha Mwana wa Mungu. : "Ninyi mnaotumaini katika Mwana wa Mungu"

Mwana wa Mungu

Hiki nicheo muhimi sana kwa Ysu ambacho uelezea uhusiano wake kwa Mungu.

uzima

Hapa "uzima" husimama badala ya haki ya kuishi milele kwa neema na upendo wa Mungu. Tazama 1:1

Na huu ndio ujasiri tulionao mbele zake, kwamba

"tuna ujasiri mbele za Mungu kwa sababu tunajua, kwamba"

kama tukiomba kitu chochote sawa sawa na mapenzi yake

"Kama tunaomba mambo ambayo Mungu hutamani"

tunajua kwamba tunacho hicho tulichomwomba.

"tunajua kwamba tutapokea ambacho tumemwomba Mungu"

1 John 5:16

ndugu

Mwamini mwenza

uzima

"uzima" hapa husimama bada ya haki ya kuishi milele kwa neema na pendo la Mungu. Tazama 1:1

Mauti

hii humanisha hauti ya milele, yaani, kutumia muda wote mbali na uwepo wa Mungu.

1 John 5:18

Sentensi Unganishi

Yohana anahitimisha barua yake, akifunua alichokisema kwa kuhusu hali mpya ya waaminio ambayo haiwezi kutenda dhambi na anawakumbusha kulinda na sanamu.

ulimwengu wote

"ulimwengu" ni njia ambayo kwayo baadhi ya waandishi wa Kibiblia huwazungumzia watu waishio watu wote wanaoishi ulimwenguni walio katika uasi dhidi ya Mungu na pia hulitumia kuelezea mfumo wa ulimwengu uliodhiliwa na nguvu ya dhambi yenye kuharibu.

chini ya utawala wa yule mwovu.

yaani, katika nguvu za yule mwovu.

1 John 5:20

Maelezo ya Jumla

Maneno "yeye" na "Aliye" humrejea Yesu Kristo

Mwana wa Mungu

Hiki ni cheo muhimu kwa Yesu ambacho huelezea uhusiano wake kwa Mungu.

ametupatia ujuzi

"ametuwezesha kumwelewa huyo kweli"

uzima

Hapa, neno "uzima" husimama kwa niaba ya haki ya kuishi milele kwa neema na pendo la Mungu. Tazama maelezo katika1:1.

Yeye ni... uzima wa milele

hili linasimama kwa niaba ya wazo kwamba Kristo hutupatia uzima wa milele.

Watoto

Yohana alitumia maelezo haya kuonyesha kuonyesha upendo wake kwa ajili yao. : "Watoto wangu katika Kristo" au "ninyi mlio wapendwa kwangu kama watoto wangu mwenyewe." Tazama lilivyotafsiriwa katika 2:1.

Utangulizi wa 2 Yohana

Sehemu ya 1: Utangulizi wa Ujumla

Maelezo ya Kitabu cha 2 Yohana

  1. Salamu (1:1-3)
  2. Kutia moyo na amri kubwa (1:4-6)
  3. Onyo kuhusu walimu wa uongo (1:7-11)
  4. Salamu kutoka kwa waumini wenzake (1:12-13)

Nani aliandika Kitabu cha 2 Yohana?

Barua haina jina la mwandishi. Mwandishi alijitambulisha mwenyewe kama "mzee." Barua hii pengine ilikuwa imeandikwa na Mtume Yohana alipokaribia kuaga dunia. Maudhui ya 2 Yohana inafanana na yale yaliyo katika Injili ya Yohana.

Je, kitabu cha 2 Yohana kinahusu nini?

Yohana aliandika barua hii kwa mtu aliyemwita "mwanamke aliyechaguliwa" na "watoto wake" (1:1). Hii inaweza kutaja rafiki maalum na watoto wake. Au inaweza kutaja kundi fulani la waumini au waumini kwa ujumla. Kusudi la Yohana la kuandika barua hii lilikuwa kuwaonya wasikilizaji wake kuhusu walimu wa uongo. Yohana hakutaka waumini wawasaidie au watoe fedha kwa walimu wa uongo. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

Je, kichwa cha kitabu hiki kinapaswa kutafsiriwaje?

Watafsiri wanaweza kuchagua kuita kitabu hiki kwa kichwa chake cha jadi, "2 Yohana" au "Yohana wa Pili." Au wanaweza kuchagua kichwa cha wazi, kama "Barua ya Pili Kutoka kwa Yohana" au "Barua ya Pili Aliyoandika Yohana." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-names)

Sehemu ya 2: Dhana muhimu za Kidini na za Kitamaduni

Je, ukarimu ni nini?

Ukarimu ulikuwa dhana muhimu katika Mashariki ya Karibu ya kale. Ilikuwa muhimu kuwa na urafiki kwa wageni au watu wasio wa eneo hilo na kutoa msaada kwao ikiwa wangehitaji. Yohana alitaka waumini kuonyesha ukarimu kwa wageni. Hata hivyo, hakutaka waumini kuwa wakarimu kwa walimu wa uongo.

Je, ni watu gani ambao Yohana alizungumza dhidi yao?

Watu ambao Yohana alizungumza dhidi yao huenda walikuwa wale ambao watajulikana kama Wagnostiki. Watu hawa waliamini kwamba dunia ilikuwa mbaya. Kwa kuwa waliamini kwamba Yesu alikuwa wa kiungu, walikanusha kwamba alikuwa mwanadamu kweli. Hii ni kwa sababu walidhani kuwa Mungu hangeweza kuwa mwanadamu kwa sababu mwili ni mbaya. (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#evil)

2 John 1

2 John 1:1

Sentensi Unganishi

Baada ya salamu, Yohana anawaonyesha waumini kuwa upendo na kweli vinakwenda sambamba

Maelezo ya Jumla

Kihistoria mtume Yohana amekubalika kuwa ndiye mwandishi wa barua hii. Anasema "pendaneni" hii pengine barua hii liliandikiwa kanisa.

Maelezo ya Jumla

"ninyi" na "yenu" katika barua hii yanaonyesha wingi

Maelezo ya Jumla

katika barua hii Yohana anatumia maneno "sisi" na 'yetu" ikimaanisha Yohana mwenyewe pamoja na wasomaji wake

Kutoka kwa mzee kwenda kwa mwanamke mteule na watoto wake

Barua za wakati huo zilianza na jina la mwandishi, kwa kushupisha inaweza kusomeka:- " mimi, Yohana mzee, ninaandika barua hii kwa mwanamke mteule na watoto wake"

Mzee

Ni rejea kwa Yohana, mtume na mwanafunzi wa Yesu. Anajiita mzee labda kwa sababu ya umri wake mkubwa au kwa sababu ni kiongozi kanisani.

kwa mwanamke mteule na watoto wake

Pengine hii ina maana ya kundi au kusanyiko na waumini .

ambaye nampenda katika kweli.

" Ninyi watu ninaowapenda katika kweli"

wanao ifahamu kweli

"ambao wanao fahamu ukweli kuhusu Mungu na Yesu"

Baba...Mwana

Hivi ni vyeo muhimu vinavyoelezea uhusiano kati ya Mungu na Yesu

katika kweli na upendo.

Neno "kweli" linaelezea "upendo." Pengine inamaanisha "katika upendo wa kweli"

2 John 1:4

...wewe, mwanamke, nakuandikia

Ni maneno ambayo yametumiwa katika hali ya umoja.

kama vile tu tulivyoipokea amri hii kutoka kwa Baba

"Kama vile Mungu Baba alivyo tuagiaza"

siyo kwamba nakuandikia amri mpya

" siyo kwamba nakuagiza kufanya jambo jipya"

bali ile tuliyokuwa nayo tokea mwanzo

Hapa neno "mwanzo" inamaanisha " tulipoamini kwa mara ya kwanza" kwa maneno mengine:- " lakini nawaandikia kama tulivyoagizwa na Kristo kufanya tulipoamini mara ya kwanza."

tunapaswa kupendana sisi kwa sisi.

Hii inaweza kutafisiriwa kama sentensi mpya: "Na alitupa amri kwamba tunapaswa kupendana."

Hii ndiyo ile amri, kama mlivyoisikia tokea mwanzo, kwamba mnapaswa kuenenda katika hiyo.

" Mungu amewaagiza tangu mwanzo mlipoamini mpendane"

2 John 1:7

Sentensi Unganishi

Yohana anawaonya kuhusu wazushi, na kuwakumbusha kubaki katika mafundisho ya Kristo na kujiepusha na waasi

Kwa kuwa wadanganyifu wengi wamesambaa katika ulimwengu.

"Walimu wengi wa uongo wamekwisha liacha kusanyiko" au " wadanganyifu wengi wapo ulimwenguni"

wadanganyifu wengi.

"walimu wengi wa uongo" au "wazushi"

katika ulimwengu

Hapa inaelezea kila mtu aliyeko hai katika ulimwengu huu.

Yesu Kristo alikuja katika mwili.

"Yesu alikuja katika hali ya mwili wa kibinadamu."

Huyu ndiye mdanganyifu na mpinga Kristo

" Ni wale wanaowadanganya wengine na kumpinga Kristo mwenyewe"

mpinga Kristo.

" kinyume na Kristo"

Jiangalieni wenyewe.

"Iweni macho" au " iweni waangalifu."

hampotezi mambo

"kutopoteza tuzo zenu za wakati ujao kule mbinguni."

tuzo kamili

"tuzokamili kule mbinguni"

2 John 1:9

Yeyote aendeleae mbele

Hii inaonyesha mtu anaye dai kufahamu zaidi juu ya Mungu na ukweli kuliko mtu yeyote "Yeyote anayesema kuwa anafahamu zaidi kuhusu Mungu." au " Yeyote anayeikana kweli"

hana Mungu

" si mali ya Mungu"

Yeye adumuye katika fundisho anaye Baba na Mwana

"Wale wanaofuata mafundish ya Kristo ni mali ya Baba na Mwana"

Baba na Mwana

Hivi ni vyeo muhimu vinavyoelezea uhusiano kati ya Mungu na Yesu

msimkaribishe katika nyumba zenu

Hapa ina maanisha kumkaribisha na kumtendea heshima ili kujenga uhusiano na naye.

hushiriki katika matendo yake maovu

" Hushiriki naye katika matendo yake ya uovu" au" humsaidia katika matendo yake maovu."

2 John 1:12

Sentensi Unganishi

Yohana anamalizia barua yake kwa kuonyesha shauku ya kuwatembelea na anatoa salamu kutoka kanisa jingine

Maelezo ya Jumla

Maneno "kwako" yanaonyesha umoja katika mstari wa 12. Neno "yenu" linaonyesha wingi mstari wa 13

sikutaka kuyaandika kwa karatasi na wino

Yohana hakutaka kuyaandika mambo mengi lakini alitaka kuja kuongea nao ana kwa ana.

Watoto wa dada yenu mteule

Yohana anazungumza habari ya kanisa jingine kana kwamba ni dada kwa kanisa analowaandikia na waumini wa kanisa hilo anawafananisha na watoto. Hapa inasisistiza kwamba waumini wote ni familia ya kiroho.

Utangulizi wa 3 Yohana

Sehemu ya 1: Utangulizi wa Ujumla

Maelezo ya Kitabu cha 3 Yohana

  1. Utangulizi (1:1)
  2. Kutia moyo na maelekezo ya kuonyesha ukarimu (1:2-8)
  3. Diotrefe na Demetrio (1:9-12)
  4. Hitimisho (1:13-14)

Nani aliandika Kitabu cha 3 Yohana?

Barua haina jina la mwandishi. Mwandishi alijitambulisha mwenyewe kama "mzee" (1:1). Barua hii pengine ilikuwa imeandikwa na Mtume Yohana alipokaribia kuaga dunia.

Je, kitabu cha 3 Yohana kinahusu nini?

Yohana aliandika barua hii kwa muumini mmoja aitwaye Gayo. Alimwambia Gayo awe na ukarimu kwa waumini wenzake ambao walikuwa wakisafiri kupitia eneo lake.

Je, kichwa cha kitabu hiki kinapaswa kutafsiriwaje?

Watafsiri wanaweza kuchagua kuita kitabu hiki kwa kichwa chake cha jadi, "3 Yohana" au "Yohana wa Tatu." Au wanaweza kuchagua kichwa cha wazi, kama "Barua ya Tatu Kutoka kwa Yohana" au "Barua ya Tatu Aliyoandika Yohana." (See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-names)

Sehemu ya 2: Dhana muhimu za Kidini na za Kitamaduni

Je, ukarimu ni nini?

Ukarimu ulikuwa dhana muhimu katika Mashariki ya Karibu ya kale. Ilikuwa muhimu kuwa na urafiki kwa wageni au watu wasio wa eneo hilo na kutoa msaada kwao ikiwa wangehitaji. Katika 2 Yohana, Yohana aliwakataza Wakristo kutowaonyesha ukarimu walimu wa uongo. Katika Yohana 3, Yohana aliwahimiza Wakristo kuonyesha ukarimu wageni waaminifu.

Sehemu ya 3: Masuala muhimu ya Tafsiri

Je! Mwandishi hutumuia namuna gani uhusiano wa familia katika barua yake?

Mwandishi alitumia maneno "ndugu" na "watoto" kwa namna ambayo inaweza "inaweza kuleta tatizo. Maandiko mara nyingi hutumia neno "ndugu" kutaja Wayahudi. Lakini katika barua hii, Yohana alitumia neno kuelezea Wakristo. Pia, Yohana aliwaita waumini wengine "watoto" wake. Hawa ni waumini aliowafundisha kumtii Kristo.

Yohana pia alitumia neno "Myunani" kwa njia ambayo inaweza inaweza kuleta tatizo. Maandiko mara nyingi hutumia neno "Myunani" kuwataja watu ambao si Wayahudi. Lakini katika barua hii, Yohana alitumia neno kutaja wale ambao hawakuamini Yesu.

3 John 1

3 John 1:1

Sentensi unganishi

Yohana anatuma salaam kwa Gayo

Maelezo ya jumla

Hii ni barua mtu binafsi Yohana anaituma kwa Gayo. Maneno yote ya kiwakilishi cha majina yanamtaja Gayo katika umoja.

Mzee

Ni kiwakilishi cha Yohana, mtume na mwanafunzi wa Yesu. Yeye mwenyewe anajiwakilisha kama "mzee" pengine kwa sababu ya umri wake au kwasababu ya uongozi wake wa kanisa. Jina la mwandishi linaweza kufupishwa: Mimi, Yohana mzee, ninaye andika.

Gayo

Huyu ni mshirika mwamini ambaye Yohana anamwandikia barua hii.

Ambaye ninayempenda katika kweli

"Ambaye ninampenda kweli"

Unaweza kufanikiwa katika mambo yote na kuwa na afya

"Unaweza kufanya mambo yote vizuri na kuwa na afya"

Kama na roho yako ifanikiwavyo

"Kama vile unavyoendelea vizuri kiroho"

Ndugu

"washirika waumini"

dhihirisha ushuhuda wa kweli yako, kuwa unatembea katika kweli

"aniambia kuwa unaishi kulingana na ukweli wa Mungu"

Wanangu

Yohana anazungumzia wale aliowafundisha kumwamini Yesu kama vile watoto wake. Hii inauelezea upendo wake na nia yake kwa ajili yao. Inaweza pia kuwa yeye mwenyewe aliwaongoza kumjua Bwana. "Watoto wangu wa kiroho"

3 John 1:5

Sentensi unganishi

Kusudi la Yohana la kuandika barua hii ilikuwa kumhimiza Gayo kuwa makini katika njia aliyoianza ya kufundisha Biblia; kisha anazungumzia habari za watu wawili, mmoja mwovu na mwingine mwema.

Maelezo ya Jumla

Hapa neno "sisi" linamtambulisha Yohana na wale waliokuwa pamoja naye na yawezekana linawaunganisha waumini wote.

Mpendwa

Hapa inatumika kama neno la utambulisho kwa wafuasi waumini.

Unaenenda kwa uaminifu

"Unatenda kwa uaminifu kwa Mungu" au "Umekuwa mtii kwa Mungu"

unapowahudumia ndugu na wageni

"Kuhudumia ndugu waumini na wale usiowajua"

ambao wametoa ushuhuda wa upendo wako mbele ya kanisa.

"Wageni, ambao wamewaambia waumini katika kanisa jinsi mnavyowapenda"

Unafanya vizuri kuwasafirisha

"Kwa unyenyekevu ninawaomba mpate kuwasafirisha

Kwa sababu kwa ajili ya Jina, walienda

Hapa Jina linamaanisha Yesu. Walienda kuwaambia watu wengine kuhusu Yesu.

bila kuchukua kitu chochote

Bila kupokea zawadi au misaada

wa Mataifa

Hapa watu "wa mataifa" Haimaanishi kuwa ni watu wasio Wayahudi. Inamaanisha watu wasio na tumaini kwa Yesu.

ili tuwe watenda kazi wenza kwa ajili ya kweli

"Ili kwamba tutashirikiana nao kuutangaza ukweli wa Mungu kwa watu"

3 John 1:9

Maelezo ya jumla

Neno "sisi" linamwelezea Yohana na wele waliokuwa pamoja naye bila kumjumuisha Gayo.

kusanyiko

Hapa anamtaja Gayo na kundi la waumini wanaokutana pamoja kumwabudu Mungu.

Diotrofe

Alikuwa hapo awali mmoja wa kundi la waumini waliokuwa wakikusanyika

anayependa kuwa wa kwanza miongoni mwao

"Aliyependa kuonekana kuwa wa muhimu sana miongoni mwao" au "ambaye alipenda kujifanya kama vile ni kiongozi wao"

jinsi anavyosema maneno mabaya dhidi yetu

"Jinsi anavyonena mambo mabaya kutuhusu sisi na hakika siyo ya kweli"

yeye mwenyewe

Neno "yeye mwenyewe" linamwelezea Diotrofe aliyekuwa akifanya mambo hayo.

hawapokei ndugu

hataki kuwapokea ndugu waumini"

Hata huwakataza wengine ambao wanatamani kuwakaribisha hao

"Anawazuia wale wanaotaka kuwakaribisha waumini"

na kuwafukuza watoke kwenye kusanyiko.

"Anawalazimisha kutoka kwenye kusanyiko"

3 John 1:11

Maelezo ya jumla

Hapa neno "sisi" linaelezea kuhusu Yohana na wale waliokuwa pamoja naye bila kumjumuisha Gayo.

Mpendwa

Hapa inatumika kama neno la utambulisho kwa wafuasi waumini.

usiige kilicho kibaya

"Usifuatishe mambo maovu ambayo watu wanayatenda"

bali iga kilicho chema

"Fuatisha mambo mema ambayo watu wanayatenda"

ni wa Mungu

"Yanatokana na Mungu"

hajamwona Mungu

eye si mali ya Mungu" au "Hajamwamini Mungu"

Demetrio ameshuhudiwa na wote

Wote ambao wanamfahamu Demetrio wanamshuhudia" au "Kila mwumini anayemjua Demetrio ananema mema kumhusu yeye"

Demetrio

Huyu yawezekana kuwa ni mtu ambaye Yohana anamtaka Gayo na kusanyiko lote kumkaribisha wakati wa ziara yake.

na kweli yenyewe

"Kweli yenyewe pekee inanena ukweli juu yake, kwamba ni mtu mwema"

sisi pia ni mashahidi

"Sisi pia tunanena mema yahusuyo Demetrio"

3 John 1:13

Maelezo ya jumla

Huu ni mwisho wa barua ya Yohana kwa Gayo. Anampatia mambo ya hitimisho na kuifunga kwa salaamu.

lakini sipendi kukuandikia kwa kalamu na wino

Yohana hana utashi wa kuwaandikia mambo mengine yote. Hasemi kwamba kwamba angewaandikia mambo fulani zaidi ya kalamu na wino.

ana kwa ana

"Kwa pamoja" au "kwa mmoja mmoja"

Amani iwe pamoja nawe

"Mungu aweza kukupa amani"

Marafiki wanakusalimu

"Marafiki hapa wanakusalimu

marafiki

"Rafiki zako" au "Waumini wenzako"

Utangulizi wa Yuda

Sehemu ya 1 Maelezo ya Jumla

Muhtasari wa kitabu cha Yuda

  1. Utangulizi (1:1-2)
  2. Onyo kuhusu walimu wa uongo (1:3-4)
  3. Mifano ya Agano la Kale(1:5-16)
  4. Jibu linalostahili (1:17-23)
  5. Utukufu kwa Mungu (1:24-25)

Nani aliandika kitabu cha Yuda?

Mwandishi anajitambulisha kama Yuda nduguye Yakobo. Yuda na Yakobo walikuwa ndugu wa kambo wa Yesu Kristo. Haijulikani iwapo barua hii ilipaswa kuwa ya kanisa fulani.

Kitabu cha Yuda kinahusu nini?

Yuda aliaandika barua hii kuwaonya waumini kuhusu walimu wa uongo.Yuda alinukuu mara nyingi kutoka Agano la Kale. Hii inaweza ashiria kwamba Yuda aliandikia hadhira ya Wakristo wa Kiyahudi. Barua hii na 2 Petero zina ujumbe wenye kufanana. Barua zote zinazungumzia malaika, Sodoma na Gomorah na walimu wa uongo.

Kichwa cha kitabu hiki kitafsiriwe namna gani?

Watafsiri wanaweza kuchagua kukiita kitabu hiki kutumia kichwa chake cha kitamaduni, "Yuda." ama wanaweza chagua kichwa kinachoeleweka zaidi kama "Barua kutoka kwa Yuda" ama "Barua aliyoandika Yuda." (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-names)

Sehemu ya 2: Dhana muhimu za kidini na kitamaduni.

Ni watu gani Yuda aliwakemea?

Kuna uwezekano Yuda aliwakemea watu watajulikana kwa jina Wagnostiki. Walimu hawa waliharibu mafundisho ya maandiko matakatifu kwa manufaa yao wenyewe. Waliishi maisha maovu na wakafundisha watu kuishi hivyo .

Jude 1

Jude 1:1

maelezo ya jumla

Yuda anajitambulisha kama mwandishi wa hii barua na anawasalimu wasomaji wake. Yawezekana alikuwa kaka yake Yesu wakambo. Kuna Yuda wengine wawili katika Agano Jipya.

maelezo ya jumla

Neno "wewe" katika hii barua ya husu waKristo ambao Yuda alikuwa akiwandikia na ni katika wingi.

Yuda, mtumishi wa

Yuda ni kaka wa Yakobo. Tafsiri mbadala: "Mimi ni Yuda, mtumishi wa."

Na kaka yake na Yakobo

Yakobo na Yuda ni nusu kaka wa Yesu

wapendwao katika Mungu Baba

"Mungu baba anawapenda ninyi"

huruma na iwe kwenu na amani izidishwe

"kwenu" ina rejea kwa Wakristo wote waliopaswa kupokea barua hii.Tafsiri mbadala: "huruma, neema na upendo na uongezwe mara nyingi kwa ajili yenu."

Jude 1:3

kauli unganishi

Yuda anawapa waamini sababu yake ya kuandika hi barua

maelezo ya jumla

Neno "sisi" la muhusu yuda na waamini katika hii barua

Nilikuwa nafanya kila juhudi kuwaandikia ninyi

"Nilikuwa na shauku ya kuwaandikia ninyi"

wokovu wa kawaida

"tunashiriki wokovu uleule"

Ilinilazimu kuandika

"Nilijisikia uhitaji mkubwa kuandika" au "Nilijisikia hitaji muhimu kuandika"

kuwahimiza mshindanie kwa uaminifu kwa ajili ya imani

"kuwatia moyo kutetea mafundisho ya kweli"

kabidhiwa

Mungu alitoa mafundisho haya ya kweli"

kwa sababu watu fulani wamejiingiza kwa siri

"kwa kuwa baadhi ya watu wamekuja miongoni mwa walioamini pasipo kujijulisha wenyewe"

ambao hukumu yao ya dhambi ilikwisha andikwa tangu zamani

"zamani sana iliandikwa kwamba watu hawa watahukumiwa dhambi"

ambao hubadilisha neema ya Mungu kuwa zinaa

"ambao hufundisha kwamba neema ya Mungu inaruhusu mtu kudumu katika maisha ya dhambi ya zinaa"

ambao humkataa Mkuu wetu wa pekee na Bwana, Yesu Kristo

watu hawa hufundisha kwamba Yesu Kristo sio njia ya kweli au pekee ya kwenda kwa Mungu.

Kataa

kusema kwamba jambo fulani si kweli.

Jude 1:5

kauali unganishi

Yuda antoa mifano ya kale ya wale ambao hawakumfuata Bwana.

Ngpenda kuwakumbusha

"Ninataka ninyi mkumbuke"

mnajua kila kitu

Yuda hasa anarejea kwenye maandiko ya Musa ambayo wamekwisha kufundishwa. Tafsiri mbadala: "mnayajua maandiko ya Musa."

Bwana aliwaokoa mara moja watu kutoka nchi ya Misri

"Bwana aliwaokoa Waisraeli hapo zamani kutoka Misri"

lakini baadaye

"muda ulivyo endelea " au " baada ya jambo fulani kutokea"

enzi yao wenyewe

"nafasi zao" au "majukumu yaliowekwa kwao"

wakaacha wakazi yao maalum

"waliacha nafasi zao wenyewe"

Mungu amewaweka katika vifungo vya milele katika giza

"Mungu amewafunga malaika hawa ndani ya giza"

siku ile kuu

siku ya mwisho ambayo Mungu huukumu watu wote

Jude 1:7

katika namna ileile walijiingiza wenyewe kwenye

Sodoma na Gomora waliishi katika dhambi ya zinaa katika namna hihyo hiyo kama malaika walivyo fuata njia za uovu.

kama mifano ya wale ambao huteseka katika hukumu ya moto wa milele

Uharibifu wa watu wa Sodoma na Gomora ulifanyika mfano wa hatima ya wote wanao mkataa Mungu.

hawa pia walichafua

"Hawa" ina rejea kwa watu wanaomkataa Mungu ambao huchafua miili yao kwa uasherati kwa namna hiyo wakitupa takataka kwenye mkondo inaweza kusababisha maji kuwa mabaya kunywa.

kuhusu wenye utukufu

"kuhusu malaika wazuri wa Mungu"

Jude 1:9

maelezo ya jumla

Balaamu ni Nabii aliye kataa kulahani Israel kwa ajiili ya adui lakini akamfundisha huyo adui kuwafanya watu waoe wasio amini na wawe waabudu sanamu.

maelezo ya jumla

Kora alikuwa ni muIsraeli aliye asi uongozi wa Musa na ukuhani wa Aruni.

bishana kuhusu mwili

walibishana juu ya nani atachukua milki ya mwili. "bishana kuhusu nani angechukua milki ya mwili."

Mikaeli...hakuthubutu kuleta kinyume naye

"Mikaeli...alijizuia mwenyewe kumkemea ibilisi

hukumu au kuleta maneno ya matusi

"upinzani wa nguvu au maneno yasiyo na heshima"

Lakini watu hawa

"watu hawa" ni watu waovu waliotajwa mapema.

tusi mambo yote ambayo hawayaelewi

"kuongea pasipo heshima kinyume na chochote ambacho hawakijui maana yake"

njia ya Kaini

Kaini alimuua kaka yake Abeli.

kosa la Balaam kwa ajili ya mshahara

Balaamu alijaribu kulaani Israeli kwa ajili ya pesa.

uasi wa Kora

Kora aliasi dhidi ya uongozi wa Musa na ukuhani wa Aron.

Jude 1:12

sentensi unganishi

Yuda anatumia mifano mingi kumfafanua mtu asiye na utaua. Anawambia waamini jinsi wanvyo paswa kumtambua mtu huyu miongoni mwao.

Hawa ni wale

"Hawa" ina rejea kwa watu waovu.

miti iliyopukutika isiyo na matunda

Kama baadhi ya miti isiyozalisha matunda katika mwisho wa majira ya joto, hivyo watu hawa waovu hawana imani na kazi za haki.

bila matunda, kufa mara mbili

Kama miti ambayo imeuawa mara mbili kama vile kwa baridi usingeweza kutoa matunda, kwa hiyo watu waovu hawana thamani na hawana maisha ndani yao.

iliyong'olewa na mizizi

Kama miti ambayo imeng'olewa kwenye udongo na mizizi yake, watu waovu wametenganishwa kutoka kwa Mungu ambaye ni chanzo cha maisha.

pori la mawimbi ya bahari

Kama mawimbi ya bahari yanayosukumwa na upepo mkali, hivyo watu waovu hawakuwa na msingi wa imani na walihamishwa kwa urahisi katika mwelekeo mwingi.

yakitoa aibu yao wenyewe

Kama upepo usababishao pori la wimbi kukoroga povu chafu, hivyo watu hawa kwa kupitia mafundisho ya uongo na matendo huwa aibisha wenyewe. AT: "kama vile wimbi huleta povu na uchafu, watu hawa wanachafua wengine kwa aibu yao."

Nyota zinazo randaranda, ambao weusi wa giza umetunzwa kwa ajili yao milele

Kama vile nyota zitembeavyo angani na kufanya ugumu kuzifuata, hivyo na wewe usiwafuate watu hao.

Jude 1:14

watu hawa...kazi yao...wana

Hawa inarejea kwa watu waovu.

wa saba katika orodha ya Adamu

Kizazi cha saba kutoka kwa Adamu. Baadhi ya tafsiri husema sita katika orodha ya Adamu inategemeana kama Adamu anahesabika kama kizazi.

Tazama, Bwana

"taarifa, Bwana", au "tazama, bwana"

mambo yote magumu

"maneno yote makali"

manung'uniko, walalamikao

Watu walio na moyo usio na utii. Wanung'unikao huwa wanafanya hivi kimya kimya, Walalamikao hufanya hivi kwa uazi zaidi.

wajivunao mno

Watu wanao jisifu wenyewe ili kwamba wengine wawasikie.

Jude 1:17

Watu hawa

"Hawa wadhihaki"

wanatawaliwa na tamaa za asili

Watu hawa wanazungumziwa kama tamaa zao ni wafalme wanao watawala. "Awaachi kumkosea Mungu kwa kuendelea kufanya maovu wanayo tamani kufanya.

hufuata ... tamaa

Tamaa zisizo za kitauwa za ongelewa kama ni njia ambayo huyo mtu kaifuata.

ni wa kidunia

"wenye dharau wanajiingiza kwenye dhambi ya zinaa"

hawana Roho

Roho Mtakatifu anazungumziwa kama ni kitu ambacho watu wanaweza kumiliki.

Jude 1:20

sentensi unganishi

Yuda anawambia waamini jinsi ya kuishi na namna ya kuwa tendea wengine.

kama mjijengavyo wenyewe

Kama muwezavyo kukua imara na afya njema, ili kwamba muweze kuimarika na kukua fahamu zenu na roho katika maarifa ya Mungu

msubiri

"tunatazamia kwa shauku"

jitunzeni katika upendo wa Mungu

Kuweza ;kupokea upendo wa Mungu ya zungumziwa kama vile mtu amejihifadhi sehemu.

rehema za Bwana wetu Yesu Kristo ambayo huwapatia uzima wa milele

Hapa "rehema" ya wakilisha Yesu Kristo mwenyewe, ambaye atawaonyesha rehema zake kwa waaamini kwa kuwafanya wa ishi milele

Jude 1:22

baadhi ya watu, ambao wako katika mashaka

"baadhi ya watu, ambao bado hawajaamini kuwa Mungu ni Mungu"

wanyakueni kutoka katika moto

"ili kwamba wasije wakaenda kwenye ziwa la moto"

na kwa baadhi yao onesheni huruma kwa hofu

"na muwe wakarimu kwa wengine bali ogopeni kutenda dhambi kama wao."

mkichukia hata vazi lililotiwa doa na mwili

"chukieni hata mavazi yao, kwa sababu yamefayika kuwa machafu kwa dhambi." Wamejaa dhambi hivyo hata mavazi yanafikiriwa machafu.

Jude 1:24

sentensi unganishi

Yuda anafunga na baraka

kuwasababisha msimame mbele ya utukufu wake

Utukufu wake ni taa nzuri yenye kuwakilisha ukuu wake. "Na kukuruhusu kufurahia na kuabudu utukufu wake"

bila mawaa

Hapa dhambi ya tajwa kama uchafu kwenye mwili wa mtu au doa kwenye mwili wa mtu. "Utakapo kuwa bila dhambi"

kwake Mungu pekee mwokozi kupitia Yesu Kristo Bwana wetu

"kwa Mungu pekee, aliye tuokoa kwa lili Yesu Kristo alilifanya." Hii ya sisitiza kuwa Mungu baba pamoja na Mwana ndie Mwokozi.

utukufuu uwe kwake, ukuu, uwezo na nguvu kabla ya nyakati zote, na sasa na hata milele. Amina.

Mungu alikuwa nao, na anao, na siku zote atakuwa na utukufu, uongozi kamilifu, na utawala wa mambo yote.

Utangulizi wa Ufunuo wa Yohana

Sehemu ya 1: Utangulizi wa jumla

Muhtasari wa Kitabu cha Ufunuo wa Yohana

  1. Mwanzo (1:1-20)
  2. Barua kwa makanisa saba (2:1-3:22)
  3. Maono juu ya Mungu akiwa mbinguni na maono ya Yule Mwanakondoo (4:1-11)
  4. Mihuri saba (6:1-8:1)
  5. Baragumu saba (8:2-13:18)
  6. Waabudu wa Mwanakondoo, wafia dini na mavuno ya hasira (14:1-20)
  7. Vitasa saba (15:1-18:24)
  8. Ibaada mbinguni (19:1-10)
  9. Hukumu ya Mwanakondoo, kuangamizwa wa yule mnyama, miaka elfu moja,kuangamizwa wa shetani na hukumu ya mwisho (20:11-15)
  10. Uumbaji upya na Yerusalemu mpya (21:1-22:5)
  11. Ahadi ya Yesu ya kurudi, ushuhuda wa malaika, maneno ya kumalizia ya Yohana, Ujumbe wa Kristo kwa kanisa,Mwaliko na onyo (22:6-21)

Nani aliandika kitabu cha Ufunuo wa Yohana?

Mwandishi anajitambulisha kama Yohana. Labda huyu ni Mtume Yohana. Aliandika kitabu cha Ufunuo akiwa katika kisiwa cha Patmosi. Warumi walikuwa wamempeleka huko kuishi uhamishoni kwa sababu ya kuwafundisha watu kumhusu Yesu.

Kitabu cha Ufunuo kinahusu nini?

Yohana aliandika kitabu cha Ufunuo kuwatia moyo waumini ili wabaki waaminifu ingawa walikuwa wanateseka. Yohana alifafanua maono aliyopata kumhusu shetani na wafuasi wake wakiwapinga na kuwaua waumini. Katika maono haya, Mungu anasababisha vitu vingi vibaya kutokea duniani na kuwaadhibu watu wabaya. Kwa mwisho Yesu anamshinda Shetani na wafuasi wake. Kisha Yesu anawafariji wale waliokuwa waaminfu. Na waumini wataishi milele pamoja na Mungu katika mbingu mpya na dunia mpya.

Kichwa cha kitabu hiki kinastahili kutafsiriwa namna gani?

Watafsiri wanaweza amua kukiita kitabu hiki na mojawapo wa vichwa vyake vya kitamaduni kama, "Ufunuo," "Ufunuo wa Yesu Kristo,"Ufunuo kwa Mtakatifu Yohana," ama "Apokalipi wa Yohana."Ama wanaweza kuchagua kichwa cha kueleweka zaidi kama "Vitu alivyovionyesha Yesu Kristo kwa Yohana." (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-names)

Ni aina gani ya uandishi wa kitabu cha Ufunuo?

Yohana alitumia aina maalum ya uandishi kufafanua maono yake. Yohana anafafanua alichokiona kutumia alama nyingi. Mfumo huu wa uandishi unaitwa unabii wa alama ama fasihi ya kiapokalipti (inayozungumzia maangamizo yajayo). (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#writing-apocalypticwriting)

Sehemu ya 2: Dhana muhimu za kidini na kitamaduni

Je, matukio ya Ufunuo ni ya kipindi cha sasa ama kipindi kijacho?

Tangu wakati wa kwanza wa Ukristo, wasomi wamekuwa wakifafanua ufunuo tofauti. Wasomi wengine wanafikiri Yohana alifafanua matukio yaliyotokea nyakati zake. Wasomi wengine wanafikiri Yohana alifafanua matukio yaliyofanyika wakati wake hadi wakati Yesu atakaporudi. Wasomi wengine wanafikiri Yohana alifafanua matukio ambayo yangetokea muda mfupi kabla ya kurudi kwake Kristo.

Watafsiri hawatahitajika kuamua jinsi ya kukifafanua hiki kitabu hiki kitabu kabla ya kukitafsiri. Watafsiri waache unabii huo katika vitenzi vinavyotumika kwenye ULB.

Je, Kuna vitabu vingine kwenye Bibilia kama Ufunuo?

Hakuna kitabu kingine cha Bibilia kinachofanana na Ufunuo. Lakini aya katika vitabu vya Ezekieli, Zakaria na hasa Danieli zina mafundisho na aina sawa ya uandishi kama Ufunuo. Itakua na umuhimu kukitafsiri Ufunuo wakati sawa na Danieli kwa sababu vitabu hivi vina tamathali sawa za usemi na namna ya uandishi.

Sehemu ya 3: Maswala muhimu ya kitafsiri

Je, mtu anahitajika kukifahamu kitabu cha Ufunuo ili kukitafsiri?

Mtu hahitaji kufahamu alama zote katika kitabu cha Ufunuo ili kukitafsiri ipasavyo. Watafsiri wasitoe maana ya alama ama nambari katika tafsiri zao. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#writing-apocalypticwriting)

Maswala ya "takatifu" na "takasa" yameakilishwa vipi katika Ufunuo ndani ya ULB?

Maandiko yanatumia maneno haya kuashiria mojawapo ya wawazo. Kwa sababu hii, ni vigumu kwa watafsiri kuyatumia vyema katika matoleo yao. Wakati wa kutafsiri Ufunuo kwa Kiingereza, ULB hufuata sheria zifuatazo:

UDB itakuwa ya msaada kwa watafsiri kwa mara nyingi jinsi ya kuakiisha mawazo haya katika matoleo yao wenyewe.

Vipindi vya muda

Yohana aliashiria vipindi vingi vya muda katika Ufunuo. Kwa mfano kuna uashiriaji mwingi wa miezi arobaini na mbili, miaka saba, na miaka mitatu na nusu. Wasomi wengine wanafikiri vipindi hivi ni alama ya kitu fulani.Wasomi wengine wanafikiri kwamba hivi ni vipindi vya ukweli vya muda. Watafsiri wanatakikana kuvichukulia hivi vipindi kama vinavyoashiria vipindi kamili vya muda. Ni juu ya mtafsiri kuamua umuhimu wavyo ama vitu vinavyowakilishwa na vipindi hivi.

Ni maswala gani ya muhimu ya utafsiri katika kitabu cha Ufunuo?

Yafuatayo ni maswala muhimu ya uandishi katika Kitabo cha Ufunuo.

lakini ULB, UDB na matoleo mengi ya kisasa hayafanyi hivyo."

(See: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/jit.html#translate-textvariants)

Revelation 1

Ufunuo 01 Maelezo kwa jumla

Muundo na mpangilio

Sura hii inaelezea jinsi kitabu hiki ni kumbukumbu ya maono Yohana alipokea katika kisiwa cha Patmosi.

Tafsiri zingine zinaingiza ndani kidogo nukuu kutoka Agano la kale. ULB hufanya hivi na nukuu kutoka 1:7.

Dhana muhimu katika sura hii

Makanisa saba

Barua hii iliandikiwa makanisa saba halisi katika nchi inayotiwa sasa Uturuki.

Nyeupe

Rangi nyeupe huashiria utakatifu ama uadilifu katika maandiko. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#holy and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#righteous)

Tamathali muhimu za usemi katika sura hii

"Yeye aliye, Aliyekuwepo, na atakayekuja"

Maneno haya yanaeleza kwamba Mungu amekuwepo, yupo sasa na atakuwepo milele. Siyo lugha zote zina njia ya kutafsiri kwa urahisi kipindi kilichopita, kipindi cha sasa na kipindi kijacho kwa kitenzi.Inaonekana huu ni mnyambuliko wa jina la Mungu, Yahweh, lenye maana "Mimi niko".

Damu yake

Hii inaashiria kifo cha Yesu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metonymy)

Maswala mengine ya utata katika tafsiri ya sura hii.

"Anakuja na mawingu"

Wasomi wengi wanaamini kwamba Yesu atarudi kwa awamu mbili. Kurudi kwa kwanza kwa Yesu kutakua wa kisiri kama "Mwizi wa usiku." Halafu Mungu atakuja kwa njia ya uwazi ambapo kila mtu atamuona. Huu ndio ujio wa mwisho uzungumzao kitabu cha Ufunuo.

Yesu

Taswira ya yule mwanaume aliye mbinguni ni ya Yesu. Kwa mtazamo wa jumla, taswira hii ni maelezo kuhusu Yesu katika utukufu yake. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#glory na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

"Malaika wa makanisa saba"

Neno la Kigiriki linalotafsiriwa kama "malaika" linaweza kutafsiriwa pia kama "wajumbe." Kuna uwezekano hii inaashiria wajumbe ama viongozi wa makanisa haya saba.

| >>

Revelation 1:1

Taarifa ya Jumla:

Huu ni utangulizi wa kitabu cha Ufunuo. Unaeleza kuwa ni ufunuo kutoka kwa Yesu Kristo na unawabariki wote wausomao.

watumishi wake

Hii humaanisha watu wamwaminio Kristo

Nini lazima kitokee hivi punde

"matukio ya lazima kutokea hivi punde"

Kufanywa kujulikana

"kufanywa mawasiliano"

Kwa mtumishi wake Yohana

Yohana aliandika kitabu hiki na alikuwa akijitaja yeye mwenyewe: "kwangu, Yohana, mtumishi wake"

Neno la Mungu

Hii humaanisha ni ujumbe Yohana aliopewa na Mungu.

Yule anayesoma kwa sauti

Hii haihusishi mtu bayana. Inahusisha mtu yeyote anayesoma kwa sauti. "Yeyote anayesoma kwa sauti"

Tii kilichoandikwa ndani

"amini kilichoandikwa humo na kutii amri zilizomo"

Muda umekaribia

"vitu ambavyo lazima vitokee vitatokea karibuni"

Revelation 1:4

Taarifa ya Jumla:

Huu ni mwanzo wa barua ya Yohana. Hapa ajitaja kama mwandishi na kuwasalimu watu anaowaandikia.

neema iwe kwenu na amani kutoka kwake aliyepo...na kutoka kwa roho saba...na kutoka kwa Yesu Kristo

Haya ni matamanio au baraka. Yohana anazungumza kana kwamba hivi ni vitu ambavyo Mungu anaweza kugawa, ingawa ni njia ambazo anatumaini Mungu atawatendea watu wake. "Yule aliyepo...na roho saba...na Yesu Kristo awatendee kwa huruma na kuwawezesha kuishi kwa amani na usalama."

Kutoka kwake aliyepo

"kutoka kwa Mungu, aliyepo"

Atakayekuja

Atakayekuwapo baadaye ananenwa kama anayekuja.

roho saba

Namba saba ni alama ya ukamilifu na utimilifu. "Roho saba" humaanisha mojawapo kati ya Roho ya Mungu au roho saba zinazomtumikia Mungu.

Mzaliwa wa kwanza wa waliokufa

"mtu wa kwanza kufufuliwa kutoka mautini"

ametuweka huru

"ametukomboa"

ametufanya kuwa ufalme, makuhani

"ametuweka kando na kuanza kututawala na kutufanya makuhani"

Mungu na Baba yake

Huyu ni mtu mmoja. "Mungu na Baba yake"

Baba

Hili ni jina muhimu la Mungu linaloeleza uhusiano kati ya Mungu na Yesu.

kwake kuwa utukufu na nguvu

Haya ni matamanio au baraka. Maana zinazowezekana ni 1)"Watu waheshimu utukufu wake na nguvu" au 2) "awe na utukufu na nguvu". Yohana anaomba kwamba Yesu Kristo ataheshimiwa na ataweza kutawala kabisa juu ya kila mtu na kila kitu.

nguvu

hii inaweza kumaanisha mamlaka yake kama mfalme.

Revelation 1:7

Taarifa ya Jumla:

Katika mstari wa 7, Yohana ananakiri kutoka kitabu cha Danieli na Zekaria.

Kila jicho

Kwa kuwa watu huona kwa macho, neno "jicho" limetumika kuashiria watu. "kila mtu" au "watu wote"

pamoja na wote waliomchoma

"na wale waliomchoma pia watamuona"

waliomchoma

Mikono na miguu ya Yesu ilichomwa wakati aliposulibiwa msalabani. Hapa inamaanisha watu wakimuua. "walimuua"

mchoma

kutengeneza tundu katika

Alfa na Omega

Hizi ni herufi za kwanza na mwisho katika alfabeti ya Kigriki. Maana zinazowezekana ni 1) "yule aliyeanzisha vitu vyote na anayevileta mwisho vitu vyote" au 2)"yule ambaye alikuwepo na ataendelea kuwepo". "Yeye ni A na Z" au "mwanzo na mwisho"

ambaye anakuja

Atakayekuwapo baadaye ananenwa kama anayekuja.

asema Bwana Mungu

Baadhi ya lugha huweka "Bwana Mungu asema" mwanzoni au mwishoni mwa sentesi nzima.

Revelation 1:9

Taarifa ya Jumla:

Yohana anaeleza jinsi maono yake yalivyoanza na maelekezo aliyopewa na Roho.

yenu...nanyi

Hii humaanisha waumini katika makanisa saba

anayeshiriki pamoja nanyi katika mateso na ufalme na uvumilivu thabiti ulio katika Yesu

"aliye na fungu katika ufalme wa Mungu. Ninateseka pia na kuvimilia majaribu pamoja nanyi kwa sababu sisi ni mali ya Yesu"

kwa sababu ya neno la Mungu

"kwa sababu niliwaambia wengine kuhusu neno la Mungu"

katika Roho

Yohana anazungumzia kuvutwa na Roho ya Mungu kana kwamba alikua katika Roho. "kushawishika na Roho" au "Roho alinishawishi"

siku ya Bwana

siku ya kuabudu kwa waumini wa Kristo

sauti ya juu kama ya tarumbeta

Sauti ilikua na sauti kuu sana ikafanana na tarumbeta

tarumbeta

Hii humaanisha chombo cha kutengeneza muziki au kuwaita watu kwa ajili ya tangazo au mkutano.

kwenda Smirna, kwenda Pergamo, kwenda Thiatira, kwenda Sardi, kwenda Philadelphia, na kwenda Laodikia

Haya ni majina ya miji uliko Asia ambayo ni Uturuki ya leo

Revelation 1:12

Kauli unaganishi:

Yohana anaanza kueeleza alichokiona katika maono.

sauti ya nani

hii humaanisha mtu anayezungumza. "ambaye"

Mwana wa Adamu

Huu msemo unaelezea umbo la binadamu, mtu anayefanana na binadamu.

mkanda wa dhababu

kipande cha nguo kilichovaliwa kifuani. Inawezekana kuwa ilikua na nyuzi za dhahabu ndani yake.

Revelation 1:14

Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu nyeupe kama theluji

Sufu na theluji ni mifano ya vitu ambavyo ni viupe sana. Kurudiwa kwa "nyeupe kama" huonesha msisitizi kuwa zilikua nyeupe mno.

sufu

Haya na manyoya ya kondoo au mbuzi. Zilikua zinajulikana kuwa nyeupe mno.

macho yake yalikuwa kama mwali wa moto

Macho yake yanaelezwa kuwa na mwanga kama mwali wa moto. "macho yake yaling'ara kama mwali wa moto"

Nyayo zake zilikuwa kama shaba iliyosuguliwa sana

Shaba hung'arishwa kuifanya ingae na kurudisha mwanga. "Miguu yake iling'ara sana kama shaba iliyosuguliwa"

kama shaba iliyosuguliwa sana, kama shaba ambayo imekwisha pitishwa katika moto

Shaba ilisafishwa kwanza kisha kusuguliwa. "Kama shaba iliyosafishwa kwenye tanuu la moto na kusuguliwa"

tanuu

chombo imara kwa ajili ya kutunzia moto mkali sana. watu huweka vyuma ndani yake na ule moto huunguza takataka zote zilizomo katika chuma.

sauti ya maji mengi yanayotiririka kwa kasi

Hii ina sauti kuu sana kama sauti ya mto mkubwa unaotiririka kwa kasi, maporomoko ya maji, au ya mawimbi yenye sauti kali baharini.

kinywani mwake kulikuwa na upanga mkali

Ubapa wa upanga ulikuwa unchomoza kinywani mwake. Upanga wenyewe haukua ukisogea.

upanga mkali wenye makali kuwili

Hii humaanisha upanga wenye makali mawili, ambao umechongeka pande zote ili kukata pande zote.

Revelation 1:17

nikaanguka miguuni pake

Yohana alilala chini akitazama ardhi. Inawezekana alikuwa ameogopa sana na alikuwa akimpa Yesu heshima.

Akaweka mkono wake wa kulia juu yangu

"Alinigusa na mkuno wake wa kulia"

Mimi ni wa kwanza na wa Mwisho

Hii inamaanisha uasili wa Yesu wa milele.

ninazo funguo za mauti na kuzimu

Kuwa na nguvu juu ya jambo au kitu huzungumziwa kama kuwa na funguo zake. Maana inayooneshwa ni kwamba anaweza kuwapa uhai wale waliokufa na kuwatoa kuzimu. "Nina nguvu juu ya kifo na kuzimu" au "nina uwezo wa kuwapa uhai waliokufa na kuwatoa kuzimu".

Revelation 1:19

Kauli unaganishi:

Mwana wa Adamu aendelea kuzungumza

nyota

Hizi nyota ni ishara. Zinaonekana kuashiria wale malaika saba na makanisa saba.

vinara vya taa

Vinara vya taa ni ishara zinazomaanisha makanisa saba.

malaika wa yale makanisa saba

Maana zinazowezekana ni 1) malaika wa mbinguni wanaolinda yale makanisa saba au 2) wajumbe binadamu katika makanisa saba.

makanisa saba

Hii humaanisha makanisa saba ambayo yalikuwepo Asia ndogo wakati huo.

Revelation 2

Ufunuo 02 Maelezo kwa Jumla

Muundo na mpangilio

Sura ya 2 na ya 3 pamoja zinaunda kitenge kimoja.Hii sehemu mara nyingi hujulikana kama "barua saba kwa makanisa saba."Mtafsiri anaweza amua kuzitenganisha barua hizi moja kwa nyingine ili kuzitofautisha.

Tafsiri zingine zinaingiza ndani kidogo nukuu kutoka Agano la kale. ULB hufanya hivi na nukuu kutoka 2:27

Dhana muhimu katika sura hii

Umaskini na Utajiri

Sura hii inatoa maana mbili ya kuwa maskini na kuwa tajiri.Waefeso walikuwa maskini wa kifedha kwa sababu hawakuwa na pesa nyingi. Hawakuwa maskini wa kiroho kwa sababu ya "utajiri mwingi" waliokuwa nao ndani ya Kristo. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#spirit)

"Shetani ako karibu kufanya"

Kitabu cha Ufunuo kinahusu mambo ambayo Shetani atakuja kuyafanya duniani. Hata hivyo kinahusu kile ambacho Mungu atafanya mwishowe kumshinda Shetani.

Balaamu, Balaki na Jezebeli

Haya mafundisho juu ya Balaamu ni ngumu kuyaelewa iwapo vitabu vya Wafalme havijatafsiriwa. Kuna uwezekano kwamba hii inaashiria kuongoza watu wa Israeli kwa uzinzi na kwa kuabudu miungu wa uongo. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#falsegod)

Tamathali muhimu za usemi katika sura hii

Mfano

Wasomi wengine wanachukulia sura ya 2 na 3 kama mfano. Wanaelewa kama makanisa haya ni aina ya makanisa ama vipindi vya kihistoria vya kanisa. Ni vema kutafsiri hii kama maelekezo ya makanisa ya kale katika miji hii. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

"Kama una sikio, sikia kile Roho anawaambia makanisa"

Maneno haya ni mwito wa kutubu kwa watu walio ndani ya kanisa. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#repent)

Maswala mengine ya utata katika tafsiri ya sura hii

"Malaika wa makanisa saba"

Neno la Kigiriki "Malaika" linaweza pia kutafsiriwa kama "wajumbe."Kuna uwezekano hii inaashiria wajumbe ama viongozi wa makanisa haya saba.

"Haya ni maneno yake yule"

Haya maneno yanatumika kutanguliza barua hizi. Kuna uwezekano kama inaashiria Yesu. Kila barua basi inafafanua kipengele juu ya Yesu ambacho ni muhimu kwa barua nzima.

<< | >>

Revelation 2:1

Taarifa ya Jumla:

Huu ni mwanzo wa ujumbe wa Mwana wa Adamu kwa malaika wa kanisa la Efeso.

malaika

Maana zinazowezekana ni 1) malaika wa mbinguni anayelinda kanisa au 2) mjumbe binadamu kwa makanisa.

nyota

Hizi nyota ni ishara. Zinaonekana kuashiria wale malaika saba na makanisa saba.

Vinara vya taa

Vinara vya taa ni ishara zinazomaanisha makanisa saba.

Najua ... bidii yako ya kazi na uvumilivu wako thabiti

"Bidii" na "uvumilivu" ni nomino dhahania na zinaweza kutafsiriwa na kitenzi "fanya kazi" na "vumilia". Ninajua ... kwamba mnafanya kazi sana na unavumilia"

na kumbe siyo

"lakini sio mitume"

na wameonekana kuwa waongo

"umetambua kuwa kuwa hao watu ni mitume wa uongo"

Revelation 2:3

kwa sababu ya jina langu

"kwa sababu unaamini jina langu" au "kwa sababu unaniamini"

na haujachoka bado

Kuvunjwa moyo inazungumziwa kama kuwa na uchovu. "haujavunjika moyo" au "haujakata tamaa"

nililonalo dhidi yako

"sikukubali kwa sababu hii" au "nina hasira na wewe kwa sababu hii"

umeuacha upendo wako wa kwanza

Kuacha kufanya kitu inazungumziwa kama kukiacha nyuma. Upendo unazungumziwa kama kitu ambacho kinaweza kuachwa nyuma. "umeacha kunipenda kama ulivyokuwa ukinipenda mwanzoni"

Kwa hiyo kumbuka ulipoanguka

Kutokupenda kama hapo mwanzo inazungumziwa kama kuanguka. "kiasi gani mlivyobadilika" au "jinsi gani mlivyonipenda"

Usipotubu

"usipoomba msamaha"

kukiondoa kinara chako

Vinara vya taa ni ishara zinazomaanisha makanisa saba.

Revelation 2:6

Wanikolai

Watu waliofuata mafundisho ya mtu aitwaye Nikolai

Mwenye sikio asikie

Kuwa tayari kusikiliza inazungumziwa kama kuwa na sikio. "Acha ambaye yuko tayari kusikiliza asikilize" au "kama uko tayari kusikiliza, sikiliza"

Na kwa yule ashindaye

Hii humaanisha mtu yeyote atakayeshinda. "yeyote atakayekataa uovu" au "kwa wale ambao hawatakubali kufanya uovu"

paradiso ya Mungu

"Bustani ya Mungu". hii ni ishara ya mbinguni.

Revelation 2:8

Taarifa ya Jumla:

Huu ni mwanzo wa ujumbe wa Mwana wa Adamu kwa malaika wa kanisa la Smirna.

Smirna

Hili ni jina la mji ulioko Asia ambayo ni Uturuki ya leo.

mwanzo na mwisho

Hii humaanisha asili ya milele wa Yesu.

Nayajua mateso yako na umasikini wako

"Mateso" na "umasikini" zinaweza kutafsiriwa kama vitenzi. "ninajua ulivyoteseka na jinsi gani ulivyo masikini"

na uongo wa wale wanaojiita ni wayahudi

"uongo" unaweza kutafsiriwa kama kitenzi. "Ninajua jinsi gani wale wanaojiita wayahudi walivyowasema vibaya" au "Ninawajua wale wanaojiita wayahudi na wamesema vitu vibaya juu yenu"

lakini siyo

"lakini sio wayahudi wa kweli"

sinagogi la Shetani

Watu wanaokusanyika kumtii au kumtukuza Shetani awnazungumziwa kama sinagogi, mahali pa wayahudi pa kuabudu na kufundishia.

Revelation 2:10

Ibilisi anataka kuwatupa baadhi yenu gerezani

"Ibilisi atasababisha hivi punde wengine wawaweke baadhi yenu gerezani"

Iweni waaminifu hadi kufa

"Kuweni waaminifu kwangu hata kama watawaua". Matumizi ya neno "hadi" haimanishi kuwa uache kuwa mwaminifu wakati wa kifo.

taji

"taji la ushindi." Hili lilikua shada ambalo asili yake ilikua ya matawi ya mizeituni au majani ya laurusi ambayo yaliweka kwenye kichwa cha mwanariadha mshindi.

taji la uzima

Maana zinazowezekana ni 1)"taji linaloonesha kuwa nimekupa uzima wa milele" au 2)"uzima wa kweli kama dhawabu kama taji la mshindi"

Mwenye sikio asikie

Kuwa tayari kusikiliza inazungumziwa kama kuwa na sikio. "Acha ambaye yuko tayari kusikiliza asiklize" au "kama uko tayari kusikiliza, sikiliza"

Yeye ashindaye

hii humaanisha mtu yeyote atakayeshinda. "yeyote atakayekataa uovu" au "kwa wale ambao hawatakubali kufanya uovu"

hatapata madhara ya mauti ya pili

"hatapitia kifo cha pili" au "hatakufa mara ya pili"

Revelation 2:12

Taarifa ya Jumla:

Huu ni mwanzo wa ujumbe wa Mwana wa Adamu kwa malaika wa kanisa la Pergamo.

Pergamo

Huu ni mji ndani ya Asia ambapo ni Uturuki ya leo.

upanga mkali, wenye makali kuwili

Hii humaanisha upanga wenye makali mawili, ambao umechongeka pande zote ili kukata pande zote.

kiti cha enzi cha shetani

Maana zinazowezekana ni 1) nguvu ya Shetani na ushawishi wake juu ya watu, au 2) mahali ambapo Shetani hutawala.

wewe walishika sana jina langu

Kuwa na imani dhabiti inazungumziwa kama kushikilia kwa nguvu. "Unaniamini kwa dhabiti"

hukuikana imani yako iliyo kwangu

"Imani" inaweza kutafsiriwa kama kitenzi "kuamini". "hukuacha kuniamini"

Antipasi

Hili ni jina la mtu.

Revelation 2:14

Lakini nina mambo machache dhidi yako

"sikukubali kwa sababu ya vitu vichache ulivyofanya" au "nina hasira na wewe kwa sababu ya vitu vichache ulivyofanya"

washikao mafundisho ya Balaamu

Maana zinazowezekana ni 1)"wafundishao alichofundisha Balaamu" au 2)"wanaofanya alichofundisha Balaamu".

Balaki

Hili ni jina la mfalme.

aliyemfundisha Balaki kuweka vikwazo mbele ya wana wa Israel

Jambo linalowapelekea watu kutenda dhambi huzungumziwa kama jiwe barabarani ambalo watu hujikwaa nalo. "aliyemuonesha Balaki jinsi ya kuwafanya watu wa Israeli kutenda dhambi".

Uasherati

"kutenda dhambi ya zinaa".

Wanikolai

Hili ni jina la kundi la watu waliofuata mafundisho ya mtu aitwaye Nikolai

Revelation 2:16

Basi tubu

kwa hiyo tubu

usipofanya hivyo

"usipotubu"

nitafanya vita dhidi yao

"kupigana dhidi yao"

kwa upanga utokao katika kinywa changu

Hii humaanisha upanga katika 1:14. Ingawa alama za lugha za ufunuo kawaida hazitakiwi kutafsiriwa, watafsiri wanaweza kuchagua kama waifafanue hii alama kama alama ya neno la Mungu, kama UDB ilivyofanya. Hii alama inaonesha kwamba Kristo atawashinda maadui zake kwa kutoa amri tu.

Mwenye sikio na askie

Kuwa tayari kusikiliza inazungumziwa kama kuwa na sikio. "Acha ambaye yuko tayari kusikiliza asikilize" au "kama uko tayari kusikiliza, sikiliza"

Yeye ashindaye

Hii humaanisha mtu yeyote atakayeshinda. "yeyote atakayekataa uovu" au "kwa wale ambao hawatakubali kufanya uovu"

Revelation 2:18

Taarifa ya Jumla:

Huu ni mwanzo wa ujumbe wa Mwana wa Adamu kwa malaika wa kanisa la Thiatra.

Thiatra

Hili ni jina la mji ndani ya Asia ambapo ni Uturuki ya leo.

Mwana wa Mungu

Hili ni jina muhimu la Yesu Kristo.

macho yake kama mwali wa moto

Macho yake yanaelezwa kuwa na mwanga kama mwali wa moto. "macho yake yaling'ara kama mwali wa moto"

nyayo kama shaba iliyosuguliwa

Shaba hung'arishwa kuifanya ingae na kurudisha mwanga. "Miguu yake iling'ara sana kama shaba iliyosuguliwa"

upendo wako na imani na huduma na uvumilivu wako thabiti

Hizi ni nomino dhahania ambazo zinaweza kutafsiriwa na vitenzi. "jinsi unavyopenda, kuamini, kuhudumu na kuvumilia kwa thabiti.

upendo wako na imani na huduma na uvumilivu wako thabiti

Maana ya mambo ya hivi vitenzi vinaweza kuweka bayana. "jinsi unavyonipenda na wengine, unavyoniamini, unavyohudumia wengine, na kustahamili tabu kwa uvumilivu".

Revelation 2:20

Lakini ninalo hili dhidi yako

"Lakini sikubali baadhi ya vitu ulivyofanya" au "Lakini nina hasira na wewe kwa sababu ya jambo ulilofanya".

mwanamke Yezebeli

Yesu alimzungumzia mwanamke mmoja kanisani mwao kana kwamba alikua Malkia Yezebeli kwa sababu alifanye vitendo vya dhambi kama vile alivyofanya Malkia Yezebeli zamani kabla ya huo wakati.

Nilimpa muda wa kutubu

"Nilimpa nafasi ya kutubu" au "nilisubiri atubu"

Revelation 2:22

Nitamtupa kwenye kitanda cha maradhi

Yeye kulazimika kulala kitandani itakua matokeo ya yesu kumfanya kuwa mgonjwa sana. "Nitamfanya alale kitandani akiumwa" au "nitamfanya aumwe sana"

na wale watendao uzinzi naye kwenye mateso makali

Yesu anazungumzia watu kuteseka kama kuwatupa katika mateso. "na nitawafanya watakaozini naye kuteseka sana"

Kuzini

"kufanya uzinzi"

hadi watakapotubu dhambi zao

"kama hawatatubu dhambi zake anazozifanya".

Nitawapiga wanawe wafe

"Nitawaua watoto wake"

watoto wake

Yesu alizungumzia wafuasi wake kama vile walikuwa watoto wake. "wafuasi wake" au "watu wanaofanya anachofundisha"

mawazo na mioyo

Neno "moyo" mara nyingi humaanisha hisia na tamaa. Haya mawazo mawili yaweza kutafsiriwa kama vitenzi. "nini ambacho watu wanawaza na kutaka".

Nitampa kila mmoja wenu

Huu ni udhahiri kuhusu adhabu na thawabu. "Nitawaadhibisha au kuwazawadia kila mmoja wenu"

Revelation 2:24

kwa wale wote msioshika fundisho hili

Kuamini fundisho inazungumziwa kama kulishika fundisho. "watu wote wasioamini fundisho hili"

fundisho hili

jina "fundisho" linaweza kutafsiriwa kama kitenzi. "anachofunza"

mafumbo ya Shetani

"vitu vya kina afundishavyo Shetani"

vitu vya kina

Vitu vya siri huzungumziwa kama vile ni vya kina. "vitu vya siri"

baadhi huita mafumbo ya Shetani

Maana zinazowezekana ni 1) wale walioviita vitu vya kina walielewa kuwa vilitoka kwa Shetani au 2) watu wengine waliviita vitu vya kina lakini Yesu alichokua anasema ni kwamba ni vya kutoka kwa Shetani. "vitu vya Shetani, ambavyo baadhi ya watu huita vitu vya kina"

Revelation 2:26

Yule ashindaye

Hii humaanisha mtu yeyote atakayeshinda. "yeyote atakayekataa uovu" au "kwa yule ambaye hatakubali kufanya uovu"

Atawatawala ... atawavunja vipande

Huu ni utabiri kutoka Agano la Kale kuhusu mfalme wa Israeli, lakini Yesu alimaanisha hapa kwa wale atakaowapa mamlaka juu ya mataifa.

Atawatawala kwa fimbo ya chuma

Kutawala kwa ukali kunazungumziwa kama kutawala kwa fimbo ya chuma. "Atawatawala kwa ukali kama vile anawapiga na fimbo ya chuma."

kama mabakuli ya udongo, atawavunja vipande vipande

Kuwavunja katika vipande ni picha inayoonesha 1) kuwateketeza watenda maouvu au 2)kuwashinda maadui. "Atawashinda kabisa maadui wake kama vile kuvunja vipande vipande mabakuli ya udongo."

Kama nilivyopokea kutoka kwa Baba yangu

Lugha zingine zinaweza kuhitaji kuonesha kilichopokelewa. Maana zinazowezekana ni 1)"Kama vile nilivyopokea mamlaka kutoka kwa Baba yangu" au 2) Kama nilivyopokea nyota ya asubuhi kutoka kwa Baba yangu.

Baba yangu

Hili ni jina muhimu la Mungu linaloeleza mahusiano kati ya Mungu na Yesu.

nitampa pia

Hapa inamaanisha yule atakaye shinda.

nyota ya asubuhi

Hii ni nyota inayoonekana asubuhi kabla ya kupambazuka. Ilikua pia ni ishara ya ushindi.

Mwenye sikio asikie

Kuwa tayari kusikiliza inazungumziwa kama kuwa na sikio. "Acha ambaye yuko tayari kusikiliza asikilize" au "kama uko tayari kusikiliza, sikiliza"

Revelation 3

Ufunuo 03 Maelezo kwa jumla

Muundo na mpangilio

Sura ya 2 na ya 3 zinaunda kitenge kimoja. Sehemu hii mara nyingi hujulikana kama "barua saba kwa makanisa saba."Mtafsiri anaweza amua kuzitenganisha barua hizi moja kwa nyingine ili kuzitofautisha.

Tafsiri zingine zinaingiza ndani kidogo msitari wa ushairi ili isomeke kwa urahisi. ULB hufanya hivi na ushairi ulioko katika 3:7

Dhana muhima katika sura hii.

Roho saba za Mungu

Maana halisi ya maneno haya haiko wazi. Kuna uwezekana kama hii inaashiria Roho Mtakatifu na nambari saba inaashiria "ukamilifu". Inawezekana pia kama inaashiria roho saba ambazo zinazunguka kiti cha enzi cha Mungu. Sio ya lazima kufafanua hili kwenye tafsiri.

Nyota saba

Kuna uwezekano kama hii inaashiria viongozi wa makanisa. (Tazama:Ufunuo 1:20)

Tamathali muhimu za usemi katika hii sura

Mfano

Wasomi wengine wanachukulia sura ya ya 2 na ya 3 kama mfano. Wanaelewa haya makanisa kama aina ya makanisa ama vipindi vya kihistoria vya kanisa.Ni vyema kutafsiri hii kama maelekezo ya makanisa ya kale katika miji hii. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

Maneno,"Tazama, nasimama mlangoni na kubisha" ni mfano mungine inayoelezea utayari na kukubali kwake Yesu kumpokea mtu yeyote anayetubu na kumuamini. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#repent and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#believe)

"Kama una sikio, sikia kile Roho anawaambia makanisa"

Maneno haya ni mwito wa kutubu kwa watu walio ndani ya kanisa.

Maswala mengine ya utata katika tafsiri ya sura hii

"Malaika wa makanisa saba"

Neno la Kigiriki "Malaika" linaweza pia kutafsiriwa kama "wajumbe."Kuna uwezekano hii inaashiria wajumbe ama viongozi wa makanisa haya saba.

"The words of the one who"

The verses with these words can be difficult to translate. They do not make complete sentences. You may need to add "These are" to the beginning of these verses. Also, Jesus used these words to speak of himself as if he were speaking of another person. Your language may not allow people to speak of themselves as if they were speaking of other people. Jesus began speaking in Revelation 1:17. He continues to speak through the end of Chapter 3.

<< | >>

Revelation 3:1

Taarifa ya Jumla:

Huu ni mwanzo wa ujumbe wa Mwana wa Adamu kwa malaika wa kanisa la Sardi.

Sardi

Hili ni jina la mji ndani ya Asia ambayo ni Uturuki ya leo.

roho saba

Namba saba ni alama ya ukamilifu na utimilifu. "Roho saba" humaanisha mojawapo kati ya Roho ya Mungu au roho saba zinazomtumikia Mungu.

nyota saba

Nyota hizi ni alama. Zinaonekana kuasharia wale malaika saba wa makanisa saba.

hai ... mfu

Kumtii na kumheshimu Mungu inazungumziwa kama kuwa hai; kutomtii na kutomheshimu inazungumziwa kama kuwa mfu.

Amka

Kuwa makini na hatari inazungumziwa kama kuamka. "Kuwa makini" au "kuwa mwangalifu"

kuimarisha yaliyosalia, lakini yako karibu kufa

Matendo mema yaliyofanywa na waumini wa Sardi yanazungumziwa kama vile yako hai lakini yako hatarini kufa. "kamilisha kazi iliyosalia au kile ulichokifanya hakitakua na maana" au "kama hautakamilisha ulichoanza kufanya, kazi yako ya nyuma itakua batili"

Revelation 3:3

yale uliyoyapokea na kusikia

Hii humaanisha neno la Mungu ambalo waliamini. "neno la Mungu mlilosikia na ukweli mlioamini"

usipoamka

Kuwa makina na hatari huzungumziwa kama kuamka. "Kuwa makini" au "Kuwa mwangalifu."

nitakuja kama mwivi

Yesu atakuja wakati watu hawatarajii kama vile mwizi ajavyo asipotarajiwa.

majina machache ya watu

Hii humaanisha watu wenyewe. "watu wachache"

hawakuchafua nguo zao

Yesu anazungumzia dhambi katika maisha ya mtu kama vile ni nguo chafu. "hawajafanya maisha yao yawe yenye dhambi kama nguo chafu"

Watatembea pamoja nami

Watu kawaida walizungumzia kuishi kama "kutembea."

wamevaa nguo nyeupe

Nguo nyeupe huashiria maisha masafi bila dhambi. "na watavikwa nguo nyeupe ambayo inaonesha waso ni wasafi"

Revelation 3:5

Yeye ashindaye

Hii humaanisha mtu yeyote atakayeshinda. "yeyote atakayekataa uovu" au "kwa wale ambao hawatakubali kufanya uovu"

atavikwa mavazi meupe

Hii inaweza kutafsiriwa na kitenzi. "atavaa mavazi meupe" au " Nitampa ngu nyeupe"

nitalitaja jina lake

Hata taja jina lake tu bali atatangaza kuwa huyu ni mtu wake. "Nitatangaza kuwa ni mali yangu"

Baba yangu

Hili ni jina muhimu la Mungu linaloeleza uhusiano kati ya Mungu na Yesu.

Mwenye sikio asikie

Kuwa tayari kusikiliza inazungumziwa kama kuwa na sikio. "Acha ambaye yuko tayari kusikiliza asikilize" au "kama uko tayari kusikiliza, sikiliza"

Revelation 3:7

Taarifa ya Jumla:

Huu ni mwanzo wa ujumbe wa Mwana wa Adamu kwa malaika wa kanisa la Filadefia.

ufunguo wa Daudi

Yesu anazungumzia mamlaka yake kuamua nani aingie katika ufalme wake kama vile ni ufunguo wa Mfalme Daudi.

hufungua na hakuna afungaye

"anafungua mlango wa ufalme na hakuna awezaye kuufunga.

hufunga na hakuna awezaye kufungua

"hufunga mlango na hakuna awezaye kuufungua"

nimekuwekea mbele yako mlango uliofunguliwa

"Nimekufungulia mlango"

jina langu

neno "jina" mara nyingi hutumika kuonesha mtu mwenye hilo jina. "mimi"

Revelation 3:9

sinagogi la Shetani

Watu wanaokusanyika kumtii au kumtukuza Shetani wanazungumziwa kama sinagogi, mahali pa wayahudi pa kuabudu na kufundishia.

kusujudu

Hii ni ishara ya unyenyekevu, sio kuabudu. "Sujudu kwa unyenyekevu"

mbele ya miguu yako

"mbele yako"

watajua

"watajifunza" au "watakiri"

nitakulinda pia katika saa ya kujaribiwa

"nitakutunza pia katika saa ya kujaribiwa"

saa ya kujaribiwa

"muda wa kujaribiwa." Hii inaweza kumaanisha "wakati ambapo watu watajaribu kukufanya usinitii.

inakuja

Iliyo siku za usoni inazungumziwa kama ijayo.

Naja upesi

Inaeleweka kuwa anakuja ili ahukumu. "Ninakuja kuhukumu hivi punde"

Shikilia sana

"Endelea kuamini"

taji

Taji ilikua ni shada ambalo asili yake ilikua ya matawi ya mizeituni au majani ya laurusi ambayo yaliweka kwenye kichwa cha mwanariadha mshindi.

Revelation 3:12

yeye ashindaye

hii humaanisha mtu yeyote atakayeshinda. "yeyote atakayekataa uovu" au "kwa wale ambao hawatakubali kufanya uovu"

nguzo katika hekalu la Mungu wangu

"Nguzo" inaonesha kuwa sehumu muhumi na ya kudumu katika ufalme wa Mungu. "imara kama nguzo katika ufalme wa Mungu wangu"

Mwenye sikio asikie

Kuwa tayari kusikiliza inazungumziwa kama kuwa na sikio. "Acha ambaye yuko tayari kusikiliza asikilize" au "kama uko tayari kusikiliza, sikiliza"

Revelation 3:14

Taarifa ya Jumla:

Huu ni ujumbe wa Mwana wa Adamu kwa malaika wa kanisa la Laodikia.

Maneno yake aliye Amina

Hape "aliye Amina" ni jina la Yesu Kristo. Athibitisha ahadi za Mungu kwa kusema amina.

mtawala juu ya uumbaji wa Mungu

Maana zinazowezekana ni 1)"yule ambaye antawala vitu vyote vilivyoumbwa na Mungu" au 2)"yule ambaye Mungu aliumba vitu vyote kupitia kwake."

wewe si baridi wala moto

"Baridi" na "moto" inaonesha kuvutiwa kwa mambo ya kiroho au kumpenda Mungu kwa pande mbili tofauti kabisa. Kuwa "baridi" ni kuwa kinyume kabisa na Mungu na kuwa wa "moto" ni kuwa na uchu wa kumtumikia.

vuguvugu

"joto kidogo." Hii humuelezea mtu aliye na hamu ndogo ya mambo ya kiroho.

nitakutapika utoke kinywani mwangu

Kuwakataa inazungumziwa kama kuwatapika kutoka kinywani. "Nitawakataa kama vile nitemavyo maji ya uvuguvugu."

Revelation 3:17

wewe ni duni sana, wakuhuzunikiwa, maskini, kipofu na uchi

Yesu anazungumzia hali yao ya kiroho kama vile anazungumzia hali yao ya kimwili. "Nyie ni kama watu duni sana, wakusikitisha, maskini, vipofu, na uchi."

Nunua kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto

Dhahabu iliyo safishwa katika moto ni safi na ya dhamani sana. Hapa wokovu ambao Yesu anawapa binadamu unazungumziwa kama dhahabu. "Pokeeni kutoka kwangu kilicho cha dhamani zaidi kama vile ni dhahabu iliyotakaswa katika moto."

upate kuwa tajiri

Hii humaanisha utajiri wa kiroho, kuishi maisha yenye dhamani sana mbele za Mungu. "wawe matajiri kiroho" au "aishi maisha ya dhamani zaidi"

nguo nyeupe za kumetameta

Nguo nyeupe zinaonesha utakatifu. "utakatifu kama nguo nyeupe"

upate kuona

Kuona inamaanisha kuelewa ukweli.

Revelation 3:19

kuwa mkweli na utubu

"kuwa makini na utubu"

nasimama katika mlango na kubisha

Yesu anazungumzia watu kutaka kuhusiana naye kama vile wanataka kumkaribisha nyumbani mwao. "Mimi ni kama yule asimamaye mlangoni akibisha hodi"

na kubisha

Watu hubisha hodi wakitaka kukaribishwa kwenye nyumba ya mtu. "na ninataka mniruhusu niingie ndani"

asikiaye sauti yangu

Msemo wa "sauti yangu" huonesha Yesu akizungumza. "anayesikia nikizungumza" au "anayesikia nikiita"

nitakuja na kuingia nyumbani kwake

Lugha zingine zinaweza kupendelea kitenzi cha "nenda". "Nitaenda nyumbani kwake"

na kula naye

Hii huonesha kuwa pamoja kama marafiki.

Revelation 3:21

Kauli unganishi:

Huu ni mwisho wa ujumbe wa Mwana wa Adamu kwa malaika wa makanisa saba.

Yeye ashindaye

hii humaanisha mtu yeyote atakayeshinda. "yeyote atakayekataa uovu" au "kwa wale ambao hawatakubali kufanya uovu"

ukaa chini pamoja nami juu ya kiti changu cha enzi

Kukaa katika kiti cha enzi humaanisha kutawala. "kutawala pamoja nami" au "kuketi na mimi katika kiti changu cha enzi na kutawala na mimi"

Baba yangu

Hili ni jina muhimu la Mungu linaloeleza mahusiano kati ya Mungu na Yesu.

Mwenye sikio asikie

Kuwa tayari kusikiliza inazungumziwa kama kuwa na sikio. "Acha ambaye yuko tayari kusikiliza asikilize" au "kama uko tayari kusikiliza, sikiliza"

Revelation 4

Ufunuo 04 Maelezo kwa jumla

Muundo na mpangilio

Tafsiri zingine zinaingiza ndani kidogo msitari wa ushairi ili isomeke kwa urahisi. ULB hufanya hivi na ushairi ulioko katika 4:8,11

Sura hii inaanzisha sehemu iliyobaki ya kitabu cha Ufunuo na ni tofauti na sura tatu za kwanza. Inaelezea kufumbuliwa kwa picha Yohana anaona kwenye maono yake.

Dhana muhimu katika sura hii

Utukufu

Sura hii yote ni picha inayofafanua onyesho fulani mbinguni ambapo kila kitu kinampatia Mungu utukufu kila wakati. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#heaven and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#glory)

Mifano muhimu ya usemi katika sura hii

Mfano

Ufafanuzi wa mtu akaliaye kwenye kiti cha enzi una mifano nyingi sana. Tamaduni nyingi hazina haya mawe maalum ya thamani na kuna uwezekano yanaashiria kitu fulani chenye umuhimu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-simile and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-unknown)

Maswala mengine ya utata katika tafsiri ya sura hii.

Picha ngumu

Kuna picha nyinga ambazo zisizo wezekana kuwa ngumu ama zisizoezekana.Kwa mfano,mwanga utokapo kwenye kiti cha enzi, taa ambazo ni roho saba za Mungu "ama mfano wa bahari iliyo mbele ya kiti cha enzi.Ni vyema kuacha ugumu huu kubaki katika tafsiri yako. (Tafsiri: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#writing-apocalypticwriting)

<< | >>

Revelation 4:1

Taarifa ya Jumla:

Yohana aanza kueleza maono yake ya kiti cha enzi cha Mungu.

Baada ya mambo haya

"baada ya vitu ambavyo Yohana ametoka kuona"

mlango ulikuwa umefunguliwa mbinguni

Msemo huu humaanisha uwezo ambao Mungu alimpa Yohana kuona mbinguni, angalau kwa njia ya maono.

ikizungumza nami kama tarumbeta

Jinsi sauti ilikuwa kama tarumbeta inaweza kuainishwa vizuri. "kuzungumza na mimi kwa sauti kama sauti ya tarumbeta"

tarumbeta

Hii humaanisha chombo cha kutengeneza muziki au kuwaita watu kwa ajili ya tangazo au mkutano.

nilikuwa katika Roho

Yohana anazungumzia kuvutwa na Roho ya Mungu kana kwamba alikua katika Roho. "kushawishika na Roho" au "Roho alinishawishi"

yaspi na akiki

Mawe ya thamani. Yaspi inawezekana ilikua nyeupe kama kioo

zumaridi

Jiwe la thamani la kijani

Revelation 4:4

wazee ishirini na wanne

wazee wanne -"wazee 24"

taji za dhahabu

Hizi zilikua kama mashada ya matawi ya mizeituni na majani ya laurusi zilizopondwa katika dhahabu. Taji za naamna hii za majani walipewa wanariadha washindi vichwani mwao.

miale ya radi

Mwanga unaotokea wakati radi ikipiga.

muungurumo ya radi

Hii ni miungurumo ya sauti ambayo radi husababisha.

roho saba

Namba saba ni alama ya ukamilifu na utimilifu. "Roho saba" humaanisha mojawapo kati ya Roho ya Mungu au roho saba zinazomtumikia Mungu.

Revelation 4:6

bahari ya kioo

Inaainisha wazi jinsi ilivyokua kama kioo au bahari. Maana zinazowezekana ni 1) bahari linazungumziwa kama vile ni kioo. "bahari lililo laini kama kioo" au 2) kioo kinazungumziwa kama vile ni bahari. "kioo kilichosambazwa kama bahari"

kama kioo

Inaainishwa wazi jinsi ilivyokua kama kioo. "nyeupe kama kioo"

Katikati ya kiticha enzi na kukizunguka

"Hapo hapo karibu na kiti cha enzi" au "Karibu na kiti cha enzi na kukizunguka"

wenye uhai wanne

"viumbe wanne" au "vitu vinne vyenye uhai"

Revelation 4:7

Kiumbe hai

"kiumbe hai" au "kitu hai".

wamejaa macho juu na chini

Juu na chini ya kila bawa kulijaa macho.

atakayekuja

Aliyepo wakati wa usoni azungumziwa kama ajaye

Revelation 4:9

aliyekuwa ameketi kwenye hicho kiti cha enzi, yeye aishiye milele

Huyu ni mtu mmoja. Yule ambaye ameketi kwenye kiti cha enzi anaishi milele na milele.

milele na milele

Maneno haya yana maana moja na yanarudiwa kuonesha msisitizo. "milele yote"

wazee ishirini na wanne

wazee wanne -"wazee 24"

walisujudu wenyewe

Kulala chini kwa kutazama ardhi.

kutupa chini taji zao mbele ya kiti cha enzi

Hizi zilikua mfano wa taji za matawi ya mizeituni au majani ya laurusi yaliopondwa katika dhahabu. Mifano ambayo iliundwa kwa majani walipewa wanariadha washindi kuvaa kichwani. Wazee walikua wakionesha kuwa wanatii utawala wa Mungu. "walitupa chini mataji yao mbele ya kiti cha enzi kuonesha kumtii yeye"

Bwana wetu na Mungu wetu

"Bwana wetu na Mungu." Huyu ni mtu mmoja yule ambaye ameketi kwenye kiti cha enzi.

kupokea utukufu na heshima na nguvu

Hivi ni vitu ambavyo Mungu anavyo siku zote. Kusifiwa kuwa navyo inazungumziwa kama kuvipokea. "kusifiwa kwa utukufu wake, heshima, na nguvu" au "kwa kila mmoja kumsifu kwa sababu yeye ni mtukufu, mwenye heshima, na mwenye nguvu.

Revelation 5

Ufunuo 05 maelezo kwa jumla

Muundo na mpangilio

Tafsiri zingine zinaingiza ndani kidogo msitari wa ushairi ili isomeke kwa urahisi. ULB hufanya hivi na ushairi ulioko katika 4:8, 11

Dhana muhimu katika sura hii

Kitabo kilichofungwa na mihuri

Katika kitabu kilichofungwa na mihuri kimeandikwa ujumbe uliofichwa ambao unangojelewa kusomwa. Kitabu hiki kinaweza kusomwa tu na mtu aliye na mamlaka ya kukifungua.

Wazee ishirini na wanne

Labda maneno haya yanaashiria viongozi wa kanisa lakini utambulisho ya wazee ishirini na wanne sio na hakika. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#writing-apocalypticwriting)

Sala za Kikristo

Sala za Wakristo zimeunganishwa na ubani. Sala za Wakristo zina harufu nzuri kwa Mungu. Mungu anafurahi wakati Wakristo wanapoomba.

Roho saba za Mungu

Maana halisi ya maneno haya haiko wazi. Kuna uwezekano kama ni mfano inayoashiria Roho Mtakatifu na nambari saba ikiashiria "ukamilifu." Kuna uwezekano kwamba pia si mfano, lakini inaashiria roho saba zinazozunguka kiti cha enzi cha Mungu.

Mifano muhimu ya usemi katika sura hii

Mfano

"Simba wa kabila la Yuda" na "mzizi wa Daudi" inaashiria Yesu. Hizi ni mifano inayotumika kama vyeo vya Yesu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

<< | >>

Revelation 5:1

Kauli unganishi:

Yohana anaendelea kueleza alichokiona katika maono ya kiti cha enzi cha Mungu.

Kisha nikaona

"Baada ya kuona hivyo vitu ,nikaona"

yule aliyekuwa amekaa katika kiti cha enzi

Hii ni sawa sawa na "moja" kama 4:1

gombo lililoandikwa mbele na nyuma

"gombo linye maandishi mbele na nyuma"

lilikuwa limetiwa mihuri saba

"lilikuwa limefungwa na mihuri saba"

Nani astahiliye kulifungua gombo na kuzivunja mihuri yake?

Mtu huyu atahitaji kuivunja mihuri ili kuifungua gombo. "Nani anayestahili kuvunja mihuri na kufungua gombo?"

Nani astahiliye kulifungua gombo na kuzivunja mihuri yake?

Hii inaweza kutafsiriwa kama amri. "Acha yule ambaye anastahili kufanya hivi aje avunje mihuri na kuifungua gombo!"

Revelation 5:3

mbinguni au duniani au chini ya dunia

Hii inamaanisha mahali pote: Mahali ambapo Mungu na malaika huishi, mahali ambapo watu na wanyama huishi, na mahali ambapo wale waliokufa walipo.

Tazama

"Sikiliza" au "kuwa makini na jambo nilotaka kukuambia"

Simba wa kabila ya Yuda

Hili ni jina la mtu kutoka kabila la Yuda ambaye Mungu aliahidi atakuwa mfalme mkuu. "Yule aitwaye Simba wa kabila la Yuda" au "Mfalme aitwaye Simba wa kabila la Yuda"

Simba

Mfalme anazungumziwa kama vile yeye ni simba kwa sababu simba ni mnyama imara sana.

shina la Daudi

Huyu ni mzawa wa kizazi cha Daudi ambaye Mungu aliahidi atakuwa mfalme mkuu. "yule aitwaye shina la Daudi"

shina la Daudi

Huyu mzawa anazungumziwa kama vile familia ya Daudi ni mti na yeye ni shina lake.

Revelation 5:6

Taarifa ya Jumla:

Mwanakondoo aonekana katika chumba cha kiti cha enzi

mwanakondoo

"mwanakondoo" ni mtoto wa kiume wa kondoo. Hapa hutumika kuashiria kuwa ni Kristo.

roho saba za Mungu

Namba saba ni alama ya ukamilifu na utimilifu. "Roho saba" humaanisha mojawapo kati ya Roho ya Mungu au roho saba zinazomtumikia Mungu.

zilizotumwa duniani kote

Hii inaweza kutafsiriwa na kitenzi. "kwamba Mungu alizozituma kote duniani

Akaenda

Akakaribia kiti cha enzi. Lugha zingine zitatumia kitenzi "njoo". "alikuja"

Revelation 5:8

Mwanakondoo

"mwanakondoo" ni mtoto wa kiume wa kondoo. Hapa hutumika kushiria kuwa ni Kristo.

wazee ishirini na wanne

wazee wanne -"wazee 24"

wakainama hadi nchi

Kulala chini kwa kutazama ardhi.

Kila mmoja

Maana zinazowezekana ni 1)"kila mzee ni kiumbe hai" au 2)"kila mzee"

bakuli ya dhahabu iliyojaa uvumba ambayo ni maombi ya waamini

Uvumba hapa ni alama ya maombi ya waumini wa Mungu.

Revelation 5:9

Kwa kuwa ulichinjwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "kwa kuwa waliwachinja" au "kwa kuwa watu waliwaua"

kuchinjwa

Hii inaweza kumaanisha kutolewa uhai kwa ajili ya sadaka

na kwa damu yako

Kwa sababu damu huashiria uhai wa mtu, kupoteza damu huashiria kufa. Hii inaweza kumaanisha "kwa kifo chako" au "kwa kufa kwako."

ukamnunulia Mungu watu

"Ulinunua watu ili wawe wa Mungu" au "ulilipia gharama ili watu wawe wa Mungu"

wa kila kabila, lugha, jamaa na taifa

Hii humaanisha watu kutoka kila kabila.

Revelation 5:11

elfu kumi kwa elfu kumi na elfu kwa elfu

Hii huonesha kuwa hii ni idadi kubwa sana ya watu. "mamilioni" au "maelfu mengi sana kuhesabu"

Astahili mwanakondoo

"Mwanakondoo anastahili"

kupokea uwezo, utajiri, hekima, nguvu, heshima, utukufu, na sifa

Hivi ni vitu ambavyo Mwanakondoo anavyo. Kusifiwa navyo inazungumziwa kama kuvipokea. "kusifiwa kwa utukufu wake, utajiri, hekima, nguvu, heshima, utukufu."

Astahili .. kupokea ... sifa

Hii inamaanizha kuwa anastahili kusifiwa na kila mtu.

Revelation 5:13

mbinguni na duniani na chini ya nchi

Hii inamaanisha mahali pote: Mahali ambapo Mungu na malaika huishi, mahali ambapo watu na wanyama huishi, na mahali ambapo wale waliokufa walipo.

Kwake yeye aketiye juu ya kiti cha enzi na kwa mwanakondoo, kuwe sifa, heshima, utukufu

Kitenzi "toa" kinaweza kutumika kuonesha jinsi sifa, heshima na utukufu "ni" kwake yeye aliye katika kiti cha enzi na kwa Mwanakondoo. "Tunapaswa kumpa sifa, heshima, na utukufu yule aketiye kwenye kiti cha enzi na kwa Mwanakondoo"

na nguvu ya kutawala milele na milele

Kitenzi "kuwa" kinaweza kutumika kuonesha jinsi gani nguvu inaweza kuwa kwake aliye kwenye kiti cha enzi na kwa Mwanakondoo. "na wawe na nguvu kutawala milele na milele"

Revelation 6

Ufunuo 06 Maelezo ya jumla

Muundo na mpangilio

Mfano wa hasira ya Mungu katika sura hii imewekwa kutia uoga kwa wale watakayosikia maneno haya. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#fear)

Dhana muhimu katika sura hii

Mihuri saba

Kuna kutoelewana kuhusu jinsi mihuri hii imeambatanishwa kwenye kitabu.Ingekuwa ya kueleweka iwapo iliwekwa upande upande lakini kitabu kingeonyesha kilichomo baada ya muhuri wa mwisho kuvunjwa. Si hivyo sura hii inafafanua kitabu kwa sababu kila muhuri unafunua hukumu fulani. Inaaminika pia kwamba kutokuwepo kwa muhuri wa saba kunafunua baragumu saba za hukumu.(Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#judge na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#writing-apocalypticwriting)

Bei Inaongezeka

Bei ya vitu fulani vitaongezeka kwa gahfla. Watu hawataweza kununua vitu wanavyohitaji kwa kuishi. Hii ndio inaitwa "mfumuko."

Mifano muhimu ya usemi katika sura hii

Yule Mwana-Kondoo

Hii inaashiria Yesu. Katika sura hii, inatumika pia kama cheo cha Yesu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

Mifano

Mwandishi anatumia aina nyingi za mifano. Hii ni kwa sababu anajaribu kufafanua picha ya vitu anavyoona katika maono. Kwa hivyo, analinganisha picha hizi kwenye maono na mambo ya kawaida. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-simile)

<< | >>

Revelation 6:1

Kauli unganishi:

Yohana aendelea kueleza matukio yaliotokea mbele ya kiti cha enzi cha Mungu. Mwanakondoo aanza kufungua mihuri na gombo.

Njoo!

Hii ni amri kwa mtu mmoja, inavyoonekana ni mpanda farasi mweupe anayezungumziwa kwenye mstari wa 2.

akapewa taji

Hii aina ya taji ni mfano wa shada la matawi ya mizeituni na majani laurusi ambazo huwezekana zilipondwa kwenye dhahabu. Mifano ambayo iliundwa kwa majani ilipewa kwa wanariadha washindi kuvaa vichwani mwao. Hii inaweza kutafsiriwa na kitenzi. "alipokea taji" au "Mungu alimpa taji"

Taji

Hili lilikua shada la matawi ya mzeituni na majani ya laurusi kama mashada ambayo wanariadhaa washindi walivyopokea kipindi cha Yohana.

Revelation 6:3

muhuri wa pili

"muhuri unaofuata" au "muhuri namba mbili"

mwenye uhai wa pili

"mwenye uhai afuataye" au "mwenye uhai namba mbili"

mwekundu kama moto

"alikua mwekundu kama moto" au "alikua mwekundu wa kungaa"

Aliye mpanda alipewa ruhusa

Hii inaweza kuelezwa kama kitenzi. "Mungu alimpa ruhusa aliyempanda" au "aliyempanda alipokea ruhusa"

Huyu aliye mpanda alipewa upanga mkubwa

Hii inaweza kuelezwa kama kitenzi. "Huyu aliyempanda alipokea upanga mkubwa" au "Mungu alimpa upanga mkubwa yule aliye mpanda."

Revelation 6:5

muhuri wa tatu

"muhuri unaofuata" au "muhuri namba tatu"

mwenye uhai wa tatu

"mwenye uhai afuataye" au "mwenye uhai namba tatu"

mizani

Chombo kinachotumika kupima uzito wa vitu.

kibaba cha ngano kwa dinari moja

Lugha zingine zingependa kutumia kitenzi kama "gharimu" au "nunua" katika sentesi. "Kibaba cha ngano sasa kina gharimu dinari moja" au "Nunua kibaba cha ngano kwa dinari moja." Kulikuwa na ngano chache kwa watu wote kwa hiyo bei yake ilikuwa juu sana.

kibaba cha ngano

Hii huonesha kipomo bayana ambacho kilkuwa kama lita moja. "lita moja" au "bakuli moja"

dinari moja

Hii sarafu ilikua na dhamani ya mshahara wa siku nzima. "sarafu moja ya shaba" au "malipo ya siku moja ya kazi"

Lakini usiyadhuru mafuta na divai

Kama mafuta na divai yangedhuriwa, basi yangekua machache kwa ajili ya watu kununua na kwa hiyo bei zake zingepanda juu.

mafuta na divai

Hii misemo inawezekana kumaanisha uvunaji wa mafuta ya mizeituni na uvunaji wa zabibu.

Revelation 6:7

muhuri wa nne

"muhuri unaofuata" au "muhuri namba nne"

mwenye uhai wa nne

"mwenye uhai afuataye" au "mwenye uhai namba nne"

kijivu

"kijivu". Hii ni rangi ya maiti kwa hiyo ni rangi ya kuashiria kifo.

robo ya nchi

robo moja ya nchi - Nchi hapa inaonesha watu wa duniani. "robo moja" ya watu duniani"

upanga

Upanga ni silaha na hapa inaashiria vita.

na kwa wanyama wa mwitu katika nchi

Hii inamaanisha kwamba mauti na kuzimu zitasababisha wanyama wa mwitu kuua watu.

Revelation 6:9

muhuri wa tano

"muhuri unaofuata" au "muhuri namba tano"

chini ya madhabahu

Hii inaweza kuwa "katika kitako cha madhabahu."

wale waliokuwa wameuawa

Hii inaweza kutafsiriwa na kitenzi. "wale ambao wameuwawa na wengine"

neno la Mungu na kutokana na ushuhuda

Maana zinazowezekana ni 1) ushuhuda ni ushahidi wa Mungu juu ya ukweli wa neno lake (kama inavyooneshwa kwenye UDB), au 2) ushuhuda ni ushahidi wa aliye amini juu ya ukweli wa neno la Mungu.

walioushika

Kuamini neno la Mungu na ushuhuda wake vinazungumziwa kama vitu ambavyo vinaweza kushikwa mikononi. "ambavyo waliamini"

ulipiza kisasi damu yetu

Neno damu hapa linaonesha vifo vyao. "adhibu waliotuuwa"

hata itakapotimia ... ambao watauawa

Hii inaonesha kuwa Mungu ameshaamua kwamba kuna idadi ya watu ambayo watauwawa na adui zao.

watumishi wenzao na ndugu zao wa kike na wa kiume

Hili ni kundi la watu linalofafanuliwa kwa njia mbili: kama watumishi na kaka na dada. "Kaka zao na dada zao wanaomtumikia Mungu pamoja nao" au "waumini wenzao wanaomtumikia Mungu pamoja nao"

ndugu zao wa kiume na wa kike

Wakristo wanazungumziwa kuwa kama ndugu wa kiume na wa kike. "Wakristo wenzao" au "waumini wenzao"

Revelation 6:12

muhuri wa sita

"muhuri unaofuata" au "muhuri namba sita"

jeusi kama nguo ya magunia

Wakati mwingine nguo za magunia zilitengenezwa na nywele nyeusi. Watu walivaa magunia walipokuwa wakiomboleza. Picha ya magunia inapaswa kuwaongoza watu kuwaza mauti na kuomboleza. "nyeusi kama nguo za kuomboleza"

kama damu

Picha ya damu inapaswa kuwaongoza watu kuwaza mauti. Jinsi ilivyokuwa kama damu inaweza kuainishwa vizuri. "nyekundu kama damu"

kama mtini upukutishavyo matunda yake ya wakati wa baridi unapotikiswa na kimbunga

"kama jinsi matunda mabichi yanvyoanguka kwa wingi kutoka mtini pale upepo mkali unapotikiswa."

Anga ilitoweka kama gombo lililoviringishwa

Kawaida anga lilifikiriwa kuwa bati gumu la chuma lakini sasa lilikuwa dhaifu kama kipande cha kartasi ambacho kinachanwa kirahisi na kukunjwa.

Revelation 6:15

majemadari

Hili neno humaanisha wapambanaji wanao amuru vitani.

mapango

Mashimo makubwa kando kando ya mlima.

uso wake

Hii humaanisha Mungu. Hawakutaka Mungu awaone na kuwaadhibu.

uso

Hapa "uso" unatumilia kuonesha wazo la "uwepo."

siku kuu ya gadhabu yao imewadia

Siku ya ghadhabu yao humaanisha ule wakati ambapo watu waovu wataadhibiwa. "hiki ndicho kile kipindi kibaya watakapowaadhibu watu"

imewadia

Iliyopo sasa inazungumziwa kama vile imefika.

gadhabu yao

"Yao" humaanisha yule aliye katika kiti cha enzi na Mwanakondoo.

nani awezaye kusimama?

Kupona au kuendelea kuwa hai vinazungumziwa kama kusimama. Hili swali linatumika kuonesha huzuni yao kuu na uuoga kwamba hakuna mtu awezaye kupona pale Mungu atakopowaadhibu. "Hakuna awezaye kupona"

Revelation 7

Ufunuo 07 Maelezo ya jumla

Muundo na mpangilio

Wasomi wengi wanaamini kwamba nusu ya kwanza ya sura hii inahusu uamusho mkuu miongoni mwa Waisraeli ambapo watu 144,000 watakuja kumuamini Yesu. Nusu ya pili ya sura hii inatuelezea uamusho mkuu miongoni mwa watu wa Mataifa ambapo watu wasiohesabika watakuja kumuamini Yesu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#believe na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#writing-apocalypticwriting)

Tafsiri zingine zinaingiza ndani kidogo msitari wa ushairi ili isomeke kwa urahisi. ULB hufanya hivi na ushairi ulioko katika 7:5-8, 15-17

Dhana muhimu katika sura hii

Kuabudu

Watu kwenye sura hii wanaitikia matukio haya kwa kutubu na kuabudu.Hiki ndicho kiitikio cha kweli cha habari iliyoko katika kitabu hiki.(Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#reveal, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#repent na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#worship)

Dhiki kuu

Hiki ni kipindi ambacho watu wa duniani wataadhibiwa vikali na Mungu. Kuna kutoelewana kuhusu kipindi hiki lakini wasomi wengi wanaamini kwamba hiki ni kipindi cha nusu ya mwisho ya miaka saba ya dhiki kuu inayotabiriwa katika Ufunuo 4-19 na katika sehemu zinginezo za maandiko.

Mifano muhimu ya usemi

Mwanakondoo

Hii inaashiria Yesu.Katika sura hii, inaashiria pia cheo cha Yesu.(Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

<< | >>

Revelation 7:1

Taarifa ya Jumla:

Yohana anaanza kueleza maono ya watumishi 144,000 wa Mungu waliotiwa muhuri. Hii inatendeka katikakati ya pale ambapo Mwanakondoo anafungua muhuri wa sita na muhuri wa saba.

kona nne za dunia

Dunia inazungumziwa kama vile ni tambarare na mraba kama kartasi. Usemi "kona nne" humaanisha kaskazini, kusini, mashariki na magharibi.

muhuri wa Mungu aliye hai

Neno "muhuri" hapa humaanisha kifaa kinachotumika kuweka alama katika muhuri wa nta. Na hapa, hiki kifaa kitatumika kuweka alama katika watu wa Mungu. "alama" au "stampu"

tumekwishaweka muhuri katika paji za vichwa

Neno "muhuri" hapa linamaanisha alama. Hii alama inaonesha kwamba hawa ni watu wa Mungu na atawalinda. "weka alama katika paji za vichwa"

paji za vichwa

Paji la kichwa ni juu ya uso, juu ya macho.

Revelation 7:4

waliotiwa muhuri

Hii inaweza kusemwa kama kitenzi. "wale ambao wamewekwa alama na malaika wa Mungu"

144,000

"watu laki moja na elfu arobaini na nne"

Elfu kumi na mbili kutoka kabila

"12,000 kutoka katika kabila"

Revelation 7:7

Kauli unganishi:

Hii inaendeleza orodha ya watu wa Israeli waliowekewa muhuri.

Revelation 7:9

Taarifa ya Jumla:

Yohana anaanza kueleza maono ya pili kuhusu umati ukimsifu Mungu. HIli ni kundi tofauti la watu na wale 144,000 waliotiwa muhuri. Hii pia inachukua nafasi kati ya Mwanakondoo alipofungua muhuri wa sita na wa saba.

umati mkubwa

"kundi kubwa" au " idadi kubwa ya watu"

kanzu nyeupe

Hapa rangi "nyeupe" inaashiria usafi.

Wokovu ni kwa

"Wokovu unatoka kwa"

Wokovu ni kwa ... Mwanakondoo

walikuwa wakimsifu Mungu na Mwanakondoo. Nomini "wokovu" inaweza kuelezwa na kitenzi "kuokoa." "Mungu wetu aketiye katika enzi, na Mwanakondoo wametuokoa!"

Revelation 7:11

Malaika wote ... wenye uhai

"Malaika wote walisimama kuzunguka kiti cha enzi pamoja na wazee na wenye uhai wanne.

viumbe wenye uhai wanne

Hawa ni viumbe wanne waliotajwa katika 4:6

wakainama chini ardhini na wakaweka nyuso zao juu ya ardhi

"walisujudu"

Sifa, utukufu ... kwa Mungu wetu

"Mungu wetu anastahili sifa zote, utkufu, hekima, shukrani, heshima, uwezo na nguvu"

Sifa, utukufu ... shukurani, heshima ... viwe kwa Mungu wetu

Kitenzi "toa" inaweza kutumika kuonesha jinsi gani sifa, utukufu, na heshima "niza" Mungu. "Tunapaswa kumpa sifa , utukufu, shukrani, na heshima Mungu wetu"

hekima ... uwezo na nguvu viwe kwa Mungu wetu

"Mungu wetu ana hekima yote, uwezo na nguvu"

milele na milele

Haya maneno mawili yanamaana moja na yanasisitiza kuwa sifa haitaisha.

Revelation 7:13

waliovaa kanzu nyeupe

Hizi kanzu nyeupe zilionesha kuwa ni watakatifu.

waliotoka katika dhiki kuu

"wamepona katika dhiki kuu" au "wamepita katika dhiki kuu"

dhiki kuu

"kipindi cha mateso makubwa" au "kipindi ambacho watu watateseka vibaya sana"

Wamezifua kanzu zao na kuzifanya nyeupe kwa damu ya Mwanakondoo

Kufanywa mtakatifu na damu ya Mwanakondoo inazungumziwa kama kufua kanzu zao na damu yake. "Wamefanywa watakatifu kwa kufua nguo zao katika damu yake"

Wamezifua kanzu zao na kuzifanya nyeupe kwa damu ya Mwanakondoo

Neno "damu" inatumika kuonesha kifo cha Mwanakondoo. Kifo chake kinaweza kuzungumziwa vizuri. "Wamefanywa watakatifu kwa kufua nguo zao katika kifo chake"

Revelation 7:15

Kauli Unganishi:

Mzee aendelea kuzungumza na Yohana.

wako ...yao ... wao

Hizi zote zinamaanizha wale watu waliotoka katika Dhiki Kuu.

usiku na mchana

Sehemu hizi mbili na siku zinatumika pamoja kumaanisha "wakati wote" au " bila kukoma"

atasambaza hema yake juu yao

"ataweka hema yake juu yao." Kuwalinda inazungumziwa kama kuwapa hifadhi ya kuishi. "atawahifadhi" au "atawalinda"

Jua halitawachoma

Joto la jua linalinganishwa na adhabu inayosababisha watu wateseke. "Jua halitawachoma" au "Jua halitawadhoofisha"

Mwanakondoo aliye katikati ya kiti cha enzi

"Mwanakondoo anayesimama katikati ya eneo ya kiti cha enzi" au "Mwanakondoo aliye katika kiti cha enzi"

Kwa kuwa Mwanakondoo ... atakuwa mchungaji wao

Wazee wanamzungumzia Mwanakondoo kuwajali watu wake kama mchungaji anavyojali kondoo wake. "Kwa kuwa Mwanakondoo ... atakuwa kama mchungaji kwao" au " Kwa kuwa Mwanakondoo ... atawajali kama mchungaji anavyojali kondoo wake"

atawaongoza katika chemchemi ya maji ya uzima

Wazee wanakizungumzia kinachowapa uhai kama vile ni chemchemi ya maji safi. "Atawaongoza kama mchungaji awaongozavyo kondoo wake kwenye maji masafi" au "atawaongoza kuelekea maishani kama mchungaji anavyowaongoza kondoo wake kuelekea kwe maji masafi"

Mungu atafuta kila chozi katika macho yao

Machozi hapa yanawakilisha huzuni. "Mungu atafuta huzuni yao kama vile anafuta machozi yao" au "Mungu atawasababisha wasiwe na huzuni tena"

Revelation 8

Ufunuo 08 Maelezo ya jumla

Dhana muhimu katika sura hii

Mihuri saba

Kuna kutoelewana kuhusu jinsi mihuri hii imeambatanishwa kwenye kitabu.Ingekuwa ya kueleweka iwapo iliwekwa upande upande lakini kitabu kingeonyesha kilichomo baada ya muhuri wa mwisho kuvunjwa. Hivi sivyo sura hii inafafanua kitabu kwa sababu kila muhuri unafunua hukumu fulani. Inaaminika pia kwamba kutokuwepo kwa muhuri wa saba kunafunua baragumu saba za hukumu.(Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#judge na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#writing-apocalypticwriting)

Mifano muhimu ya usemi

Sauti ya kupita

Sauti ya kupita imetumika mara nyingi katika sura hii kuficha utambulisho wa anayefanya hilo tendo. Itakuwa ngumu kuakilisha hili iwapo lugha ya mtafsiri haina sauti ya kupita. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-activepassive)

Mifano

Mwandishi anatumia mifano nyingi. Hii ni kwa sababu anajaribu kufafanua mifano anayoona kwenye maono. Kwa hivyo analinganisha mifano katika maono haya na vitu vya kawaida. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-simile)

<< | >>

Revelation 8:1

Kauli Unganishi:

Mwanakondoo afungua muhiri wa saba.

muhuri ya saba

Huu ni muhuri wa mwisho katika ukurasa. "muhuri unaofuata" au " muhuri wa mwisho" au "muhuri namba saba"

wakapewa tarumbeta saba

Wote walipewa tarumbeta moja. Maana zinazowezekana ni 1) "Mungu aliwapa tarumbeta saba" au 2) "Mwanakondoo aliwapa tarumbeta saba"

Revelation 8:3

autoe

"autoe uvumba kwa Mungu kwa kuuchoma"

mkononi mwa malaika

Hii inamaanizha bakuli katika mkono wa malaika. "bakuli katika mkono wa malaika"

akalijaza moto

Neno "moto" hapa inaweza kumaanisha kuchoma makaa. "akalijaza na makaa yanayowaka" au " akalijaza na makaa ya moto"

Revelation 8:6

Taarifa ya Jumla:

Malaika saba wapiga tarumbeta saba mmoja baada ya mwingine.

Vikatupwa chini katika nchi

"Malaika alitupa mvua ya mawe na moto uliochanganyikana na damu chini duniani."

theluthi moja yake iungue, theluthi moja ya miti ikaungua na nyasi zote za kijani zikaungua

"iliunguza theluthi moja ya nchi, theluthi moja ya miti na majani yote ya kijani."

Revelation 8:8

Malaika wa pili

"Malaika afuataye" au "Malaika namba mbili"

na kitu kama mlima mkubwa uliokuwa unaungua kwa moto ukatupwa

"malaika akatupa kitu kama mlima mkubwa unaoungua moto"

Theluthi moja ya bahari ikawa damu

"Ilikuwa kama bahari iligawanywa katika sehemu tatu and sehemu moja ikawa damu"

ikawa damu

Maana zinazowezekana ni 1)"ikawa nyekundu kama damu" au 2) ilikua damu kweli kweli.

theluthi moja ya viumbe hai katika bahari vikafa

"ilikuwa kama vile viumbe vyote baharini viligawanya katika makundi matatu, na viumbe vyote katika kundi moja vikafa."

viumbe hai katika bahari

"vitu vinavyoishi baharani" au "samaki na wanyama wengine walioishi baharini"

Revelation 8:10

na nyota kubwa ikaanguka kutoka mbinguni, ikimulika kama kurunzi

"na nyota kubwa uliowaka kama tochi ilianguka toka mbinguni." Moto wa ile nyota kubwa ulifanana na moto wa tochi

tochi

kijiti kilichowashwa moto upande moja ilikutoa mwanga

Jina la nyota ni Pakanga

Pakanga ni kichaka kilicho na ladha chungu. watu walitumia kutengeneza dawa na pia waliamini kuwa ilikuwa na sumu. "Jina la nyota ni Uchungu" au "Jina la nyota ni Dawa Chungu"

ikawa Pakanga

Ladha chungu ya maji inazungumziwa ka vile ilkuwa Pakanga. "ikawa chungu kama pakanga" au "ikawa chungu"

wakafa kutokana na maji yaliyokuwa machungu

"wakafa walipokunywa maji machungu"

Revelation 8:12

theluthi moja ya jua ikapigwa

Kusababisha kitu kibaya kutokea kwa jua inazungumziwa kama kulipiga au kuligonga. Hii inaweza kuelezwa na kitenzi. "theluthi moja ya jua ikabadilishwa" au "Mungu alibadili theluthi moja ya jua"

theluthi moja ya vyote ikageuka kuwa giza

Maana zinazowezekana ni 1) "theluthi moja ya muda vilikuwa giza" au 2)"theluthi moja ya jua, theluthi moja ya mwezi na theluthi moja ya nyota vilikuwa giza"

theluthi moja ya mchana na theluthi moja ya usiku havikuwa na mwanga

"mwanga haukuwepo theluthi moja ya siku na theluthi moja ya usiku" au "havikutoa mwanga theluthi moja ya siku na theluthi moja ya usiku"

Revelation 8:13

kwa sababu ya ... tarumbeta iliyosalia ... malaika

"kwa sababu malaika ambao walikuwa bado hawajapuliza tarumbeta walitaka kuzipuliza"

Revelation 9

funuo 09 Maelezo kwa jumla

Muundo na mpangilio

Sura hii inaendeleza hukumu za baragumu saba. Hii sura na ile iliyopita inajumuisha kitengo kimoja.

Ole

Kuna aina nyingi za "ole" maalum ambazo zimetajwa katika kitabu cha Ufunuo. Sura hii ina ole hizi za kwanza. Kuna uwezekano hizi zina maana ya umuhimu wa kimuundo wa matukio kulingana na wakati katika Ufunuo.

Dhana muhimu katika sura hii

Picha ya mnyama

Mfano ya mnyama ni kawaida katika kitabu hiki na pia kwenye hii sura.Watu wa kale wa mashariki ya karibu huenda waliwatazama hawa wanyama kama wenye walikua na 'tabia fulani' iliyoakilisha wanyama hawa. Kwa mfano simba mara nyingi huonekana kama aliye na nguvu. Mtafsiri asijaribu kutoa maana ya kila picha hizi.

Shimo lisilo na mwisho

Hii ni mfano ya kawaida katika kitabu cha Ufunuo kinachoashiria kuzimu.Inasisitiza kwamba kuzima haiwezi kuepukwa. "Inaelezewa kama iliyoko chini kinyume na mbinguni inayoelezewa kama iliyo juu. Hii inasisitza kwamba hakuna mbinguni wala kuzimu hapa duniani. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#hell)

Abadoni na Apolioni

"Abadoni" ni neno la Kiebrania na neno "Apolioni" ni neno la Kigiriki. Maneno yote yanamaanisha "Mwangamizi". Yohana alitafsiri Mwangamizi neno hilo la Kiebrania kwa kuiandika na herufi za Kigiriki.Watafsiri wa ULB na UDB waliyatafsiri kutumia herufi za Kingereza. Watafsiri wanashauriwa kutafsiri maneno haya kutumia herufi za lugha kusudiwa.Kwa vile wasomaji wa asili wa Wagiriki wangeelewa maana ya "Apoloni," watafsiri wanaweza kutoa maana yake katika maelezo ya tanbihi.

Toba

Sura hii inataja dhamira ya toba. Hata ingawa kuna miujiza mingi, watu wanasemekana kuepuka toba na kubaki dhambini. Si vizuri kusahau dhamira hii ukisoma kitabo cha Ufunuo. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#repent and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin)

Mifano muhimu ya usemi katika sura hii.

Mfano

Shetani mara nyingi anafanuliwa kama malaika aliyeanguka. Sababu nyota ni mfano wa malaika katika kitabu cha Ufunuo,maneno "nyota kutoka mbinguni iliyokuwa imeanguka" huenda inaashiria Shetani. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#satan, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#writing-symlanguage na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#writing-apocalypticwriting)

Kuna Kuna mifano nyingi katika sura hii. Kazi yao ni kuonyesha picha ngumu ambazo Yohana anaona katika maono yake.Kwa hivyo mifano hii inaangazia maswala yanayowezekana kuliko kuangazia kazi ya kishairi. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-simile)

Maswala mengine ya utata katika tafsiri ya sura hii

"Wale watu ambao hawakuwa na muhuri wa Mungu"

Ikiwezekana ni vyema kutotoa maana ya maneno haya waziwazi kwa tafsiri.Wasomi wengi wanaamini muhuri ni alama iliyofanywa kuwatofautisha waumini na wasioamini wakati huu wa dhiki. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#believe and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

<< | >>

Revelation 9:1

Kauli Unganishi:

Malaika wa tano kati ya saba aanza kupiga tarumbeta

Niliona nyota kutoka mbinguni iliyokuwa imeanguka

Yohana aliona nyota ikiwa imeshakwisha anguka. Hakuiona ikianguka.

ufunguo wa shimo linaloelekea kwenye shimo lisilo na mwisho

"funguo ambao unafungua tundu la shimo lisilo na mwisho"

shimo linaloelekea kwenye shimo lisilo na mwisho

Maana zinazowezekana ni 1)"shimo" linaelezea jinsi shimo lilivyo refu na lembamba, au 2)"shimo" linamaanisha uwazi wa mwanzo wa tundu la shimo lenyewe.

shimo lisilo na mwisho

Hili ni shimo refu sana na jembamba. Maana zinazowezekana ni 1)shimo halina mwisho chini; inaendelea kwenda chini zaidi milele au 2) shimo ni refu sana hata linakuwa kana kwamba halina mwisho.

kama moshi kutoka katika tanuru kubwa

Tanuru kubwa linatoa moshi mweusi na mnene. "kama moshi mkubwa utokao kwenye tanuru kubwa"

Revelation 9:3

nzige

Wadudu wanaopaa pamoja katika makundi makubwa. Watu huwahofia kwa sababu wanaweza kula majani yote kwenye bustani na kwenye miti.

nguvu kama ile ya nge

Nge wana uwezo kuwadunga na kuwapa sumu watu na wanyama wengine. "uwezo wakudunga watu kama Nge wafanyavyo"

nge

Wadudu wadogo wenye ncha kali zenye sumu mikiani. Kudungwa nao huacha maumivu makali na yanayodumu muda mrefu.

Waliambiwa kutokudhuru majani katika nchi au mmea wowote wa kijani au mti

Nzige wa kawaida walikuwa tishio kubwa kwa watu walipokuja, waliweza kula nyasi zote na majani ya mimea na miti. Nzige hizi zilikatazwa kufanya hivyo.

isipokuwa tu watu

Neno "kudhuru" au "kuumiza" linaeleweka. "lakini kudhuru watu tu"

muhuri wa Mungu

Neno "muhuri" hapa humaanisha kifaa kinachotumika kuweka alama katika muhuri wa nta. Na hapa, hiki kifaa kitatumika kuweka alama katika watu wa Mungu. "alama ya Mungu" au "stampu ya Mungu"

paji za nyuso

paji la kichwa ni juu ya uso, juu ya macho.

Revelation 9:5

Hawakupewa ruhusa

"Hawa" inamaanisha nzige.

hao watu

watu ambao walikuwa wanang'atwa na nzige.

bali kuwatesa tu

Hapa maneno "walipewa ruhusa" yanaeleweka. "lakini walipewa ruhusa kuwatesa"

kuwatesa

"kuwafanya wateseke maumivu makali"

kuwatesa kwa miezi mitano

Nzige wataruhusiwa kufanya hivi kwa miezi mitano.

kuumwa na nge

Nge ni mdudu mdogo wenye ncha kali yenye sumu mkiani. Kudungwa naye kunaweza kusababisha maumivu makali au hata kifo.

watu watatafuta kifo

Kifo kinazungumziwa kama mtu au kitu kinachoweza kufichwa. "watu watatafuta njia ya kufa" au " watu watajaribu kujiua"

hawatakipata

"hawataweza kupata njia ya kufa" au "hawataweza kufa"

Watatamani kufa

"watataka sana kufa" au "watatamani kwamba wafe"

kifo kitawakimbia

Yohana anazungumzia kifo kama vile ni mtu au mnyama anayeweza kukimbia. "hawataweza kufa" au "hawatakufa"

Revelation 9:7

Taarifa ya Jumla:

Nzige hao hawakufanana kama nzige wa kawaida. Yohana anawazungumzia kwa kueleza jinsi gani sehemu zao zinafanana na vitu vingine.

mataji ya dhahabu

Hizi zilikuwa kama mashada ya matawi ya mizeituni au majani ya laurusi yaliyopondwa katika dhahabu. Mifano iliyotengenezwa kwa majani walipewa wanariadha washindi kuvaa vichwani.

Revelation 9:10

Walikuwa na mikia

Neno "Walikuwa" inamaanisha nzige.

na mikia inayouma kama nge

Nge ni mdudu mdogo wenye ncha kali yenye sumu mkiani. Kudungwa naye kunaweza kusababisha maumivu makali au hata kifo. "na mikia kama mikia ya nge" au "na mikia iwezayo kusababisha maumivu mabaya kama mikia ya nge"

katika mikia yao walikuwa na nguvu ya kudhuru watu kwa miezi mitano

Maana zinazowezekana ni 1) walikuwa na nguvu kwa miezi mitano kudhuru watu au 2) wataweza kuuma watu na maumivu yao yatadumu miezi mitano.

shimo lisilokuwa na mwisho

Hili ni shimo refu sana. Maana zinazowezekana ni 1)shimo halina mwisho chini; inaendelea kwenda chini zaidi milele au 2) shimo ni refu sana hata linakuwa kama vile halina mwisho.

Abadoni ... Apolioni

Majina yote yanamaanisha "maangamizi"

kuna maafa mawili yaja

Ziko katika wakati wa baadae zinazungumziwa kama zinakuja.

Revelation 9:13

Kauli Unganishi:

Malaika wa sita kati ya saba kupuliza tarumbeta.

nikasikia sauti ikitoka

Sauti inamaanisha yule aliyekuwa anazungumza. Yohana hasemi msemaji ni nani, lakini inawezekana ikawa ni Mungu. "Nilisikia mtu akizungumza"

pembe ya madhabahu ya dhahabu

Hizi ni zile zehemu zinazoendeleza kona nne za juu ya madhabahu zinazofanana na pembe.

Sauti ilimwambia

Sauti inamaanisha msemaji. "Msemaji akamwambia"

Malaika wale wanne waliokuwa wameandaliwa kwa ... mwaka huo, waliachiwa

"Malaika akawaachia wale malaika wanne waliokuwa wameaandaliwa kwa ... mwaka huo"

Malaika wale wanne waliokuwa wameandaliwa

"Malaika wanne ambao Mungu aliwaanda"

kwa saa hiyo, siku hiyo, mwezi huo, na mwaka huo

Haya maneno yanatumika kuonesha kuwa kuna muda bayana na siyo muda wowote tu. "kwa muda huo bayana"

Revelation 9:16

Taarifa ya Jumla:

Ghafla, wanajeshi 200,000,000 wajitokeza katika maono ya Yohana. Yohana sasa hazingumzi wale malaika wanne walitajwa katika mstari uliopita.

200,000,000

Njia baadhi zakueleza hii ni : "milioni mia mbili" au " elfu laki mbili" au "elfu ishirini mara elfu"

vyekundu kama moto

"alikuwa mwekundu kama moto" au "alikuwa mwekundu wa kung'aa"

njano isiyoiva

"njano kama salfa"

midomoni mwao ulitoka moto, moshi na salfa

"moto, moshi na salfa zilitoka midomoni mwao"

Revelation 9:18

Kauli Unganishi:

Yohana anaendelea kuelezea farasi na mapigo waliyoleta kwa binadamu.

Theluthi ya wanadamu

"Theluthi moja ya watu."

wa kuwa nguvu ya farasi ilikuwa katika midomo yao na katika mikia yao

Nomino "nguvu" inaweza kutafsiriwa na kivumishi. "Kwa kuwa ilikuwa midomo na mikia ya farasi aliyokuwa na nguvu sana" au "kwa kuwa ilkuwa midomo na mikia ya farasi ilyoweza kuwaumiza watu"

Revelation 9:20

wale ambao walikuwa hawajauawa na mapigo haya

"wale ambao mapigo hayakuwaua"

vitu ambavyo haviwezi kuona, kusikia au kutembea

Msemo huu unatukumbusha kuwa sanamu hazina uhai na hazistahili kuabudiwa. Lakini watu hawakuacha kuviabudu. "licha ya kwamba sanamu haziwezi kuona, kusikia, au kutembea"

Revelation 10

Ufunuo 10 Maelezo ya jumla

Dhana muhimu katika sura hii

Ngurumo saba

Haieleweki wazi kilichomaanishwa na ngurumo saba. Inakubalika kwa mtafsiri kutoelewa maneno haya na kuyatafsiri kama "ngurumo saba." (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-personification na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#writing-apocalypticwriting)

"Siri la Mungu"

Haieleweki maana ya haya maneno. Siyo siri ambayo Paulo anafafanua kwa maana ya kanisa. Labda inaashiria kitu kilichofichwa na hajulikani sasa, lakini kitakachofunuliwa kimefichika ama hakijulikani kitakachofunuliwa wakati huu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#reveal)

Mifano muhimu ya usemi katika sura hii

Mfano

Kuna Mifano nyingi zimetumika kuelezea malaika huyo mkubwa. Mifano inatumika kuelezea vitu ambavyo Yohana anaona kwa kuvilinganisha na vitu vya kawaida. Lakini, upinde wa mvua na mawingu vingeeleweka kama vitu vya kawaida sivyo mifano. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-simile)

Maswala mengine ya utata katika tafsiri ya sura hii

Vitabu vya msokoto

Kitabu cha msokoto kinachotajwa katika sura hii ni tofauti na vitabu vya msokoto vingine vilivyozungumziwa sana katika kitabu cha Ufunuo kufikia sasa. Kinaitwa "cha msokoto". Mtafsiri anatakikana kuhakikisha kwamba msomaji anafahamu kwamba kuna zaidi ya kitabu kimoja cha msokoto.

<< | >>

Revelation 10:1

Taarifa ya Jumla:

Yohana anaanza kueleza maono ya malaika mkuu akishilia gombo. Katika maono ya Yohana anaona kinachoendelea kutoka duniani. Hii inachukua nafasi katikati ya kupulizwa tarumbeta ya sita na tarumbeta ya saba.

Alikuwa amefungwa katika wingu

Yohana anamzungumzia malaika kama vile alikua amevaa wingu kama nguo yake. Huu usemi unaweza kueleweka kama sitiari. Ijapo, kwa sababu vitu vya ajabu vilonekana katika maono, inaweza kueleweka kama ukweli halisia jinsi ulivyo.

Uso wake ulikuwa kama jua

"uso wake ulikuwa unang'ara kama jua"

miguu yake zilikuwa kama nguzo za moto

"Miguu" inamaanisha nyayo zake. "Nyayo zake zilikuwa kama nguzo za moto"

aliweka mguu wake wa kulia juu ya bahari na mguu wake wa kushoto juu ya nchi kavu

"alisimama na mguu wake wa kulia baharini na mguu wake wa kushoto nchi kavu"

Revelation 10:3

Kisha alipaza sauti

"Kisha malaika akapaza sauti"

ngurumo za radi saba zikasema

Ngurumo ya radi inazungumziwa kama vile ni mtu awezaye kuzungumza. "ngurumo saba za radi zakapiga sauti kali" au "radi iliunguruma kwa sauti sana mara saba"

ngurumo saba za radi

ngurumo za radi kutokea mara saba inazungumziwa kama "radi" saba tofauti.

lakini nilisikia sauti kutoka mbinguni

Neno "sauti" humaanisha msemaji. Sio malaika. "lakini nikasikia mtu akizungumza kutoka mbinguni"

Revelation 10:5

aliinua mkono wake juu mbinguni

Alifanya hivi kuonyesha kuwa aliapa kwa Mungu.

kuapa kwa yule aishiye milele na milele

"na akamuliza yule aishiye milele na milele athibitishe"

yule aishiye milele na milele

Hapa "yule" inamaanisha Mungu.

Hakutakuwepo kuchelewa tena

"Hakutakuwa na kusubiri tena" au "Mungu hatachelewa"

ndipo siri ya Mungu itakuwa imetimizwa

"Mungu atatimiza siri yake" au " Mungu atakamilisha mpango wake wa siri"

Revelation 10:8

Kauli Unganishi:

Yohana anasikia sauti kutoka mbinguni ambayo alisikia 10:3 ikizungumza naye tena.

Sauti niliyosikia kutoka mbinguni

Neno "sauti" inamaanisha msemaji anayenena. "Yule niliyemsikia akizungumza kutoka mbinguni" au "Yule aliyezungumza na mimi kutoka mbinguni"

"niambia, nilikwenda"

Hapa inamaanisha Yohana.

iliniambia

"Malaika aliniamba"

uchungu

"chungu" au "chachu." Hii inamaanisha ladha mbaya kutoka tumboni baada ya kula kitu ambacho sio kizuri kula.

litakuwa tamu kama asali

"Itakuwa na ladha tamu kama asali"

Revelation 10:10

lugha

Hii inamaanisha watu waliozungumza hizo lugha. "jumuia za lugha nyingi" au "makundi mengi ya watu waliozungumza lugha zao" au "wazungumzaji wa lugha nyingi"

Revelation 11

Ufunuo 11 Maelezo ya jumla

Muundo na mpangilio

Tafsiri zingine zinaingiza ndani kidogo msitari wa ushairi ili isomeke kwa urahisi. ULB hufanya hivi na ushairi ulioko katika 11:15, 17-18.

ole

Kuna aina nyingi maalum za "ole" ambazo zimetajwa katika kitabu cha Ufunuo.Sura hii ina ole ya pili na ya tatu. Labda ole hizi zina maana muhimu fulani kulingana na matukio ya kitabo cha Ufunuo.

Dhana muhimu katika sura hii

Watu wa mataifa

"Watu wa mataifa katika sura hii wanaashiria watu wa mataifa wasio mcha Mungu na sio watu wa mataifa ambao ni Wakristo. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#ungodly)

Mashahidi wawili

Mashahidi hawa wawili wana umuhimu kama manabii wakati wa kipindi cha Ufunuo. Wasomi wamependekeza vitu vingi kuhusu utambulisho wa hawa wanaume wawili. Haijulikani na haina umuhimu wa kujua hawa walikuwa akina nani.Badalayake, ni asili yao isiyoangamika na ujumbe wao ambao ni muhimu na haikataliki. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#prophet)

Shimo lisilo na mwisho

Hii ni taswira ya kawaida katika kitabu cha ufunuo kinachoashiria kuzimu. Inasisitiza kwamba kuzimu haiepukiki. Inaelezewa kama iliyoko chini lakini mbinguni inayoelezewa kama iliyo juu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#hell)

Maswala mengine ya utata katika tafsiri ya sura hii

"Hawa manabii wawili waliwatesa watu walioishi duniani"

Hawa manabii wawili wanahusishwa na uharbifu mkubwa utakaosababisha hasara kubwa kwa watu duniani. Hii siyo roho mbaya mbali ni jaribio la kuwaleta watu hawa kwa toba. Lakini hawatatubu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#repent na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

"Wakati umetimia wa wafu kuhukumiwa"

Watu watahukumiwa baada ya kufa.Wale wanaomkataa Yesu watapata mateso ya milele. Lakini Wakristo watatuzwa kwa uaminifu wao walioishi maisha yao kama Wakristo. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#eternity na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faithful)

<< | >>

Revelation 11:1

Taarifa ya Jumla:

Yohana anaanza kueleza maono kuhusu fimbo ya kupimia na mashahidi wawili walioteuliwa na Mungu. Maono yalichukua nafasi kati ya kupulizwa kwa tarumbeta ya sita na tarumbeta ya saba.

Nilipewa mwanzi

"Mtu alinipa mwanzi"

Nilipewa ... Niliambiwa

Aliyepewa na aliyeambiwa anamaanishwa ni Yohana.

na wale wanaoabudu ndani yake

"na hesabu wale wanaoabudu ndani ya hekalu"

Wataukanyaga

kukifanya kitu kama vile hakina dhamani kwa kutembea juu yake.

iezi arobaini na miwili

miezi miwili - "miezi 42"

Revelation 11:3

Kauli Unganishi:

Mungu anaendelea kuzungumza na Yohana.

wamevaa magunia

"wamevaa nguo chafu za maombolezo" au "watavaa nguo zilizokwaruzwa kuonesha kuwa walikuwa na masikito sana"

Hawa mashahidi ni

Yohana anaelezea hawa mashahidi ni kina nani.

Hawa mashahidi ni miti miwili ya mizeituni na vinara viwili

"Hawa mashahidi wawili ndio waliowakilishwa na miti miwili ya mizeituni na vinara viwili"

miti miwili ya mizeituni na vinara viwili

Yohana anategemea wasomaji wake wajue kuvihusu kwa sababu nabii mwingine aliandika kuvihusu miaka mingi kabla. "miti miwili ya mizeituni na vinara viwili vinavyosemwa na maandiko"

moto hutoka vinywani mwao na kuwadhuru adui zao

Kwa sababu hii inahusu matukio ya mbeleni, inaweza kuwekwa katika wakati ujao.."moto utatoka vinywani mwao na kuwateketeza adui zao"

moto ... kuwadhuru adui zao

Moto kuwaka na kuua watu inazungumziwa kana kwamba mnyama anayeweza kuwala. "moto .. utawateketeza adui zao" au "moyo ... utawachoma kabisa adui zao"

Revelation 11:6

kufunga anga ili kwamba mvua isinyeshe

Yohana anazungumzia mbingu kama vile ina mlango unaoweza kufunguliwa na kufungwa ili mvua isipite. "kuzuia mvua isidondoke toka mbinguni"

kuipiga nchi kwa kila aina ya pigo

Yohana anazungumzia mapigo kana kwamba ni kijiti ambacho mtu anaweza kuipigia dunia. "kusababisha kila aina yamatatizo kutokea duniani"

shimo lisilo na mwisho

Hili ni shimo refu sana. Maana zinazowezekana ni 1)shimo halina mwisho chini; inaendelea kwenda chini zaidi milele au 2) shimo ni refu sana hata linakuwa kana kwamba halina mwisho.

Revelation 11:8

Miili yao

Hii inamaanisha miili ya mashahidi wawili.

katika mtaa wa mji mkuu

Mji ulikua na zaidi ya mtaa mmoja. Hii ilikuwa sehemu ya wazi ambapo watu waliweza kuwaona. "kwenye mtaa mojawapo wa mji mkuu" au "kwenye mtaa mkuu katika mji mkuu"

siku tatu na nusu

"Siku 3 kamili na nusu moja ya siku" au "siku 3.5" au "siku 3 1/2"

Bwana wao

Walimtumikia Bwana na kama yeye, watakufa katika huo mji.

hawatatoa kibali kuwekwa katika kaburi

Hii ilikuwa ishara ya dharau.

Revelation 11:10

watafurahi kwa ajili yao na kusherekea

"watafurahi kwamba mashahidi wawili wamekufa"

hata kutumiana zawadi

Hili tendo linaonesha jinsi gani watu walivyofurahi.

kwa sababu hao manabii wawili waliwatesa wale walioishi katika nch

Hii ndio sababu watu walifurahi sana kwamba mashahidi wamekufa.

siku tatu na nusu

"Siku 3 kamili na nusu moja ya siku" au "siku 3.5" au "siku 3 1/2"

pumzi ya uhai kutoka kwa Mungu itawaingia

Uwezo wa pumzi unazungumziwa kama kitu kinachoweza kuingia ndani ya watu. "Mungu atasababisha mashahidi wawili kupumua tena na kuishi"

Hofu kuu itawaangukia wale wanaowaona

Hofu inazungumziwa kama kitu kinachoweza kuwaangukia watu. "Wale watakao waona wataogopa sana"

Kisha watasikia

Maana zinazowezekana ni 1) mashahidi wawili watasikia au 2) watu watasikia kile wanachoambiwa mashahidi wawili.

sauti kuu kutoka mbinguni

Neno "sauti" inammanisha ni yule anayenena. "mtu anazungumza nao kwa sauti kuu toka mbinguni na"

ikiwaambia

"ikiwaambia mashahidi wawili"

Revelation 11:13

atu elfu saba

"Watu 7,000"

watakaobaki

"wale ambao hawatakufa" au "wale ambao bado wanaishi"

kumpa utukufu Mungu wa mbinguni

"kusema kuwa Mungu wa mbinguni ni mtukufu"

Ole ya pili imepita

"Tukio la pili baya limepita."

Ole ya tatu inakuja upesi

Kuwepo kwa kipindi cha mbele inazungumziwa kama kijacho. "Ole ya tatu itatokea punde"

Revelation 11:15

Kauli Unganishi:

Malaika wa mwisho wa wale saba anaanza kupuliza tarumbeta yake.

malaika wa saba

Huyu ni malaika wa mwisho kati ya wale saba. "malaika wa mwisho" au "malaika namba saba"

sauti kubwa zilinena mbinguni na kusema

Usemi "sauti kubwa" huwakilisha wananenaji wanaozungumza kwa sauti kubwa. "Wasemaji mbinguni wakanena kwa sauti kubwa na kusema"

Ufalme wa dunia

Hapa inamaanisha mamlaka ya kutawala ulimwengu. "Mamlaka ya kutawala dunia"

dunia

Hii inamaanisha kila mtu duniani. "kila mtu duniani"

ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake

Neno "ufalme" hapa linamaanisha mamlaka ya Bwana wetu na Kristo wake waliyonayo kutawala.

Ufalme wa dunia umeshakuwa ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo wake

"Bwana wetu na Kristo wake sasa ni watawala wa dunia"

Revelation 11:16

wazee ishirini na wanne

wazee wanne -"wazee 24"

nyuso zao zimeinama chini

Kulala chini kwa kutazama ardhi.

Mungu mwenye Nguvu, ambaye yupo na ambaye alikuwepo

Hizi zinaweza kuwa sentesi. "Wewe, Bwana Mungu, ndiye mtawala juu ya vyote. Wewe ndiye uliyepo, na wewe ndiye uliyekuwepo"

ambaye yupo

"yule aliyepo" au "yule anayeishi"

alikuwepo

"aliyekuwepo" au "yule ambaye alikuwa anaisha daima"

umetwaa nguvu yako kuu

Mungu alichofanya na nguvu yake kuu inaweza kuwekwa wazi. "umewaangamiza kwa nguvu yako wote waliokuasi"

Revelation 11:18

Kauli Unganishi:

Wazee ishirini na nne wanaendelea kumsifu Mungu.

Taarifa ya Jumla:

Maneno "yako" na "wako" yanamaanisha Mungu.

Walikasirishwa

"walikasirika sana"

ghadhabu yako imekuja

Inakuwepo katika muda wa sasa ikizungumzwa kama imeshatokea. "Upo tayari kuonyesha ghadhabu yako"

Wakati umefika

Inakuwepo katika muda wa sasa ikizungumzwa kama imeshatokea. "Wakati ni sahihi" au "Sasa ni wakati"

manabii, waamini, na wale walio na hofu ya jina lako

Orodha hii inafafanua maana ya "watumishi wako". Haya hayakuwa makundi matatu ya watu tofauti. Manabii walikuwa waamini na walimuogopa Mungu.

Revelation 11:19

sanduku la agano lake llilionekana ndani ya hekalu

"Niliona sanduku la agano lake hekaluni mwake"

miali ya radi

Mwanga unaotokea wakati radi ikipiga.

kelele, ngurumo za radi

Hii ni miungurumo ya sauti ambayo radi husababisha.

Revelation 12

Ufunuo 12 maelezo ya jumla

Muundo na mpangilio

Wasomi wengi wanaamini kwamba matukio ya sura hii ni ya kipindi kilichopita na kipindi kijacho. Mwandishi anaweza zungumzia matukio bila kusema ni kipindi gani yalitokea. Hata hivyo, Yohana anayazungumzia matukio haya kana kwamba ndio yanakaribia kutokea.

Tafsiri zingine zinaingiza ndani kidogo mshororo wa ushairi ili isomeke kwa urahisi. ULB hufanya hivi na ushairi ulioko katika 12:10-12

Dhana muhimu katika sura hii

Nyoka

Kuashiria Shetani kama nyoka inakusudiwa kumfanya msomaji kukumbuka hadithi ya majaribu katika Bustani la Edeni. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

Mifano muhimu ya usemi katika sura hii

Mfano

Mwanamke ametajwa katika mifano nyingi lakini utambulisho wake hauko wazi.Sura hii inazungumzia pia kuhusu kutokea kwa mpinga Kristu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#antichrist)

Maswala mengine ya utata katika tafsiri ya sura hii

"Ishara kuu ilionekana mbinguni"

Haieleweki iwapo hii ilionekana kwa kila mtu duniani ama ilionekana tu na Yohana katika maono yake. Mtafsiri atakuwa na utata iwapo swala hili haliko wazi. Kwa kiingereza hii hufanyika kutumia sauti ya kupita ingawa siyo kila lugha ina uwezo huu.(Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-activepassive na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#writing-apocalypticwriting)

<< | >>

Revelation 12:1

Taarifa ya Jumla:

Yohana anaanza kumuelezea mwanamke anyemuona katika maono.

Ishara kuu ilionekana mbinguni

"Ishara kuu ikatokea mbinguni" au "Mimi, Yohana, niliona ishara kuu mbinguni"

mwanamke aliyefunikwa na jua

"mwanamke aliyelivaa jua"

taji ya nyota kumi na mbili

Hii ilikuwa ni mfano wa shada la majani ya laurusi na matawi ya mizeituni, lakini zikiwa na nyota kumi na mbili.

nyota kumi na mbili

"nyota 12"

Revelation 12:3

Kauli Unganishi:

Yohana anaelezea joka lililotokea kwenye maono yake.

joka

Hili lilikuwa tambaazi kubwa kali, kama mjusi. Kwa wayahudi ilikuwa ni alama ya uovu na machafuko.

Mkia wake ulikokota theluthi moja ya nyota

"Alikokota theluthi moja ya nyota na mkia wake"

theluthi moja

"moja ya tatu"

Revelation 12:5

atayatawala mataifa yote kwa fimbo ya chuma

Kutawala kwa ukali kunazungumziwa kama kutawala kwa fimbo ya chuma. "Atawatawala kwa ukali kama vile anawapiga na fimbo ya chuma.

Mtoto wake alinyakuliwa juu kwa Mungu

"Mungu alimchukua upesi mtoto wake"

Revelation 12:7

Sasa

Yohana anatumia neno hili kubadili mwenendo wa maelezo yake kutambulisha kitu kingine kinachotokea katika maono yake.

joka

Hili lilikuwa tambaazi kubwa kali, kama mjusi. Kwa wayahudi ilikuwa ni alama ya uovu na machafuko. Joka pia linatambulika katika mstari wa 9 kama "ibilisi au Shetani"

Kwa hiyo haikuwepo tena nafasi mbinguni kwa ajili yake na malaika zake

"Kwa hiyo joka na malaika wake hawakuweza tena kukaa mbinguni"

Joka mkubwa ... akatupwa chini katika dunia ... na malaika zake wakatupwa chini pamoja naye

"Mungu alilitupa joka na malaika wake toka mbinguni na kuwatuma duniani"

ule nyoka wa zamani aitwaye ibilisi au Shetani ambaye hudanganya dunia nzima

Hii taarifa inaweza kutolewa katika sentesi tofauti baada ya taarifa ya kutupwa duniani. "Hilo joka ni nyoka wa zamani anaye danganya ulimwengu. Anaitwa ibilisi au Shetani"

Revelation 12:10

"nikasikia"

anayezungumza ni Yohana.

nikasikia sauti kubwa kutoka mbinguni

Neno "sauti" inaonesha mtu anayezungumza. "Nikasikia mtu akinena kwa sauti toka mbinguni"

sasa wokovu umekuja, nguvu

Mungu kuwaokoa watu kwa nguvu zake inazungumziwa kana kwamba wokovu wake na nguvu zake ni vitu vinavyoweza kuja. "Sasa Mungu amewaokoa watu wake kwa nguvu zake"

umekuja

"kuanza kuwepo kabisa" au "kutokea" au "kuwa kweli." Sio kwamba vitu hivi havikuwepo kabala, lakini sasa Mungu anavidhihirisha kwa sababu wakati wake kutokea "umekuja."

ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake

Utawala wa Mungu na mamlaka ya Kristo yanazungumziwa kama vile vinakuja. "Mungu atawala kama mfalme, na Kristo wake anamamlaka yote"

mshitaki wa ndugu zetu ametupwa chini

Huyu ni joka aliyetupwa chini katika 12:10

ndugu zetu

Waumini wenzao wanazungumziwa kana kwamba walikuwa ni ndugu. "waumini wenzetu"

mchana na usiku

Hizi sehemu mbili za siku zinatumika pamoja kumaanisha "wakati wote" au "bila kukoma"

Revelation 12:11

Kauli Unganishi:

Sauti kuu kutoka mbinguni inaendelea kuzungumza.

Walimshinda

"Walimshinda mshitaki"

kwa damu ya Mwanakondoo

Damu inamaanisha kifo chake. "kwa sababu Mwanakondoo amemwaga damu na kuwafia"

kwa neno la ushuhuda wao

Neno "ushuhuda" inaweza kuelezwa na kitenzi "shuhudia." Pia walioshuhudiwa wanaweza kuelezwa vizuri. "kwa yale waliyosema walivyomshuhudia Yesu kwa wengine"

hata kufa

Waumini walisema ukweli kumuhusu Yesu, licha ya kwamba walikuwa wanajua kuwa maadui zao wangeweza kujaribu kuwaua kwa sababu hiyo. "lakini waliendelea kushuhudia licha ya kwamba walijua wangeweza kufa kwa hilo"

Amejawa na hasira sana

Ibilisi anazungumziwa kana kwamba ni chombo na hasira inazungumziwa kuwa kama kimiminiko kinachoweza kuwa ndani yake. "Ana hasira sana"

Revelation 12:13

joka alitambua kuwa ametupwa chini kwenye nchi

"joka alitambua ya kwamba Mungu amemtupa nje ya mbingu na kumtuma duniani"

alimfuata mwanamke

"alimfukuza mwanamke"

joka

Hili lilikuwa tambaazi kubwa kali, kama mjusi. Kwa wayahudi ilikuwa ni alama ya uovu na machafuko. Joka linatambulika pia katika mstari wa 9 kama "ibilisi au Shetani"

wakati, nyakati na nusu wakati

"miaka mitatu na nusu"

nyoka

Hii ni njia nyingine yakumaanisha yule joka.

Revelation 12:15

nyoka

Hiki ni kiumbe kimoja na joka lilotajwa mapema katika 12:7

kama mto

Maji walitiririka toka mdomoni mwake kama mto utiririkavyo. "kwa kiasi kikubwa"

kumgharikisha

"kumuosha"

ardhi ... Ilifunua kinywa chake na kuumeza mto alioutema joka kutoka kinywani mwake

Ardhi inazungumziwa kana kwamba ni kiumbe hai, na shimo linazungumziwa kama kinywa kiwezacho kunywa maji. "Shimo likafunguka kwenye ardhi na maji yakaingia humo"

joka

Hili lilikuwa tambaazi kubwa kali, kama mjusi. Kwa wayahudi ilikuwa ni alama ya uovu na machafuko. Joka linatambulika pia katika mstari wa 9 kama "ibilisi au Shetani"

kushikilia ushuhuda kuhusu Yesu

Neno "ushuhuda" inaweza kutafsiriwa kama kitenzi. "waliendelea kushuhudia kuhusu Yesu"

Revelation 13

Ufunuo 13 Maelezo ya jumla

Muundo na mpangilio

Tafsiri zingine zinaingiza ndani kidogo msitari wa ushairi ili isomeke kwa urahisi. ULB hufanya hivi na ushairi ulioko katika 13:10 ambayo imenukuliwa kutoka Agano la Kale.

Dhana muhimu katika sura hii

Jeraha ya mauti

Wasomi wengi wanaamini huu ni unabii wa kifo cha mpinga Kristo. Wanaamini mpinga Kristo ataigiza ufufuko wa Yesu ama kuugushi. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#prophet, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#antichrist na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#resurrection)

Mifano muhimu ya usemi katika sura hii

Yule Mnyama

Wasomi wengi anaamini kwamba hii ni mfano kwa kuelezea mpinga Kristu.Hii ni muhimu kwa kuelewa kikamilifu aya hii.Hii ni kinyume na mwanakondoo ambaye anaashiria Yesu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-personification na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#writing-apocalypticwriting)

Mnyama mwingine

Wasomi wengi wanaamini kwamba huyu mnyama mwingine ni nabii ama kuhani wa mpinga Kristu. Ana uwezo wa kutenda miujiza mingi na kuwafanya watu wengi kumuabudu mpinga Kristu.

Maswala mengine ya utata katika tafsiri ya sura hii

Wanyama wasiojulikana

Sura hii inatumia idadi kubwa ya wanyama wasiojulikana.Wingi wa wanyama hawa wametumika kiishara ingawa maana yao haielezeki waziwazi. Hii itasababisha utata mkubwa kwa watafsiri. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#translate-unknown)

<< | >>

Revelation 13:1

Taarifa ya Jumla:

Yohana anaanza kueleza mnyama anayetokea katika maono yake. "nikaona" inamaanisha ni Yohana aliyeona.

joka

Hili lilikuwa tambaazi kubwa kali, kama mjusi. Kwa wayahudi ilikuwa ni alama ya uovu na machafuko. Joka linatambulika pia katika mstari wa 9 kama "ibilisi au Shetani"

Yule joka akampa nguvu zake

Joka alimfanya mnyama kuwa na nguvu kama yeye. Ingawa hakupoteza nguvu zake kwa kumpa mnyama nguvu.

nguvu ... kiti chake cha enzi, na mamlaka yenye nguvu sana ya kutawala

Hizi ni njia tatu zakumaanisha mamlaka yake, na pamoja zinasisitiza kuwa mamlaka yake walikuwa makubwa.

kiti chake cha enzi

"kiti cha enzi" hapa inamaanisha mamlaka ya joka kutawala kama mfalme. "mamlaka yake ya kifalme" au "mamlaka yake kutawala kama mfalme"

Revelation 13:3

Lakini jeraha lake likapona

"Lakini hilo jeraha lilipona"

jeraha la kusababisha mauti

"jeraha baya." Hili ni jeraha kubwa linaloweza kusababisha mtu kufa.

dunia yote

Neno "dunia" inamaanisha watu waliomo ndani yake. "watu wote duniani"

ikamfuata mnyama

"ikamtii mnyama"

joka

Hili lilikuwa tambaazi kubwa kali, kama mjusi. Kwa wayahudi ilikuwa ni alama ya uovu na machafuko. Joka linatambulika pia katika mstari wa 9 kama "ibilisi au Shetani"

alimpa mamlaka yule mnyama

"alimfanya mnyama kuwa na mamlaka kama aliyokuwa nayo yeye"

Nani kama mnyama?

Hili swali linaonesha ni jinsi gani walivyostaajabishwa na mnyama. "Hakuna aliye na nguvu kama mnyama!"

Nani atapigana naye?

Hiil swali linaonesha kiasi gani watu walihofia nguvu ya mnyama. "Hakuna mtu atakayeweza kupigana na mnyama na kushinda!"

Revelation 13:5

Mnyama akapewa ... Aliruhusiwa

"Mungu alimpa mnyama ... Mungu alimruhusu mnyama"

Mnyama akapewa mdomo ili azungumze maneno ya kujisifu na matusi

Kupewa mdomo inamaanisha kuruhusiwa kuzungumza. "Mnyama aliruhusiwa kuzungumza maneno ya majivuno na matusi"

miezi arobaini na miwili

mieezi miwili - "miezi 42"

kuongea matusi dhidi ya Mungu

"kusema maneno ya kejeli kuhusu Mungu"

akalitukana jina lake, eneo alililokuwa akiishi na wale wanaoishi mbinguni

Haya maneno yanaonesha jinsi mnyama alivyozungumza maneno ya matusi dhidi ya Mungu.

Revelation 13:7

alipewa mamlaka

"Mungu alimpa mamlaka mnyama"

kila kabila, watu, lugha na taifa

Hii humaanisha watu kutoka kila kabila wanahusika.

watamwabudu

"watamwabudu mnyama"

kila mmoja ambaye jina lake halijaandikwa ... katika Kitabu cha Uzima

maneno haya yanaweka wazi ni nani duniani atakayemwabudu mnyama. "wale ambao majina yao hayakuandikwa na Mwanakondoo ... katika Kitabu cha Uzima" au "wale ambao majina yao hayakuwemo ... katika Kitabu cha Uzima"

toka uumbaji wa dunia

"Mungu alipoumba ulimwengu"

mwanakondoo

Huyu ni mtoto wa kiume wa kondoo. Hapa hutumika kuashiria kuwa ni Kristo.

aliyechinjwa

"yule ambaye watu walimchinja"

Revelation 13:9

Taarifa ya Jumla:

Hii mistari ni mapumziko kutoka kwenye hesabu ya Yohana ya maono yake. Hapa anawaonya watu wanaosoma hesabu yake.

Ikiwa yeyote ana sikio

Kuwa tayari kusikiliza inazungumziwa kama kuwa na sikio. "Acha ambaye yuko tayari kusikiliza asikilize" au "kama uko tayari kusikiliza, sikiliza"

Ikiwa yeyote amechukuliwa

Usemi huu unamaanisha kuwa imashaamuliwa kuwa mtu atachukuliwa. Kama inahitajika, watafsiri wanaweza kusema dhahiri ni nani aliyeamua. "Kama Mungu ameamua mtu achukuliwe" au "Kama ni mapenzi ya Mungu kwamba mtu achukuliwe"

Ikiwa yeyote amechukuliwa mateka

Nomino "mateka" inaweza kutajwa na kitenzi "kamata" "Kama ni mapenzi ya Mungu kwa adui kumkamata mtu fulani"

kwenye mateka ataenda

Nomino "mateka" inaweza kutajwa na kitenzi "kamata" "adui atamkamata"

Ikiwa yeyote atauawa kwa upanga

"Kama ni mpango wa Mungu kwa adui kumuua mtu fulani kwa upanga"

kwa upanga

Upanga unaashiria vita. "vitani"

atauawa

"adui atamuua"

Huu ni mwito wa utulivu na uvumilivu na imani kwa hao walio watakatifu

"Wale waliowatakatifu ni lazima wadumu katika uvumilivu na uwaminifu"

Revelation 13:11

Kauli Unganishi:

Yohana anaanza kuelezea mnyama mwingine anayetokeza kwenye maono yake.

akazungumza kama joka

Maneno makali yanazungumziwa kana kwamba ni muungurumo wa joka. "akazungumza kwa ukali kama joka azungumzavyo"

joka

Hili lilikuwa tambaazi kubwa kali, kama mjusi. Kwa wayahudi ilikuwa ni alama ya uovu na machafuko. Joka pia linatambulika katika mstari wa 9 kama "ibilisi au Shetani"

dunia na wale walioishi wakimuabudu

"watu wote duniani"

yule ambaye jeraha lake baya limepona

"yule aliyekuwa na jeraha baya lililopona"

jeraha baya

"jeraha baya." Hili ni jeraha kubwa linaloweza kusababisha mtu kufa.

Revelation 13:13

Akafanya

"Mnyama toka katika nchi alitenda"

Revelation 13:15

Aliruhusiwa

"Mungu alimruhusu mnyama kutoka katika nchi"

kutoa pumzi katika ile sanamu ya mnyama

Hapa neno "pumzi" humaanisha uhai. "kuipa uhai sanamu"

sanamu ya mnyama

Hii ni sanamu ya mnyama wa kwanza aliyetajwa.

kusababisha wale wote waliokataa kumwabudu mnyama wauawe

"kuwaua wote waliokataa kumwabudu mnyama wa kwanza"

Pia akalazimisha kila mmoja

"Mnyama kutoka katika nchi pia akamlazimisha kila mmoja"

Ilikuwa haiwezekani kwa kila mtu kuuza au kununua isipokuwa mwenye alama ya mnyama

"watu waliweza kununua na kuuza vitu ingawa tu walikuwa na alama ya mnyama." "Aliamuru kuwa watu wangeweza kununua na kuuza vitu kama tu wana alama ya mnyama"

alama ya mnyama

Hii ilikuwa alama ya kuonesha kuwa aliyekuwa nayo alimwabudu mnyama.

Revelation 13:18

Taarifa ya Jumla:

Huu mstari ni mapumziko kutoka katika hesabu ya maono ya Yohana. Hapa anawapa onyo jingine wasomaji wa hesabu yake.

Hii inahitaji busara

"Hekima inahitajika" au "Unahitaji kuwa na busara kuhusu hili"

Ikiwa yeyote ana ufahamu

Neno "ufahamu" inaweza kutafsiriwa na kitenzi "kuelewa." "Kama yeyote anaweza kuelewa vitu hivi"

mwache aweze kufanya hesabu ya namba ya mnyama

"Anapaswa kutambua maana ya namba ya mnyama" au "anatakiwa kujua maana ya namba ya mnyama"

ni namba ya kibinadamu

Maana zinazowezekana ni 1) namba inawakilisha mtu mmoja au 2) namba inawakilisha binadamu wote.

666

"mia sita sitini na sita"

Revelation 14

Ufunuo 14 Maelezo ya jumla

Dhana muhimu katika sura hii

"Ushindi dhidi ya yule mnyama"

Huu ni ushindi katika vita vya kiroho vinavyotokea wakati huu. Ingawa vita vingi vya kiroho haviezi kuonekana, kitabu cha Ufunuo kinatupa taswira ya wakati vita vya kiroho vitatokea hadharani. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#spirit and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#writing-apocalypticwriting)

Alama ya yule mnyama

Yohana amechukua muda mrefu kwa kuzungumzia ile alama inayopewa na yule mnyama. Wasomi wengi wanaamini kwamba sura hii inafundisha kwamba wale wanapokea alama hii watapata adhabu ya milele katika kuzimu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#eternity na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#hell)

Dhana muhimu katika sura hii

Mavuno

Mavuna ni mfano ya kawaida katika maandiko. Mavuno huashiria wakati vitu vizuri hutokea. Mara nyingi hutumiwa kuashiria watu kutokea kumwamini Yesu lakini Yohana hamaanishi hivi hapa. Hapa inatumika kufafanua kumalizika kwa mipango ya Mungu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith)

<< | >>

Revelation 14:1

Kauli Unganishi:

Yohana aanza kueleza sehemu ifuatayo katika maono yake. Kuna waumini 144,000 wanaosimama mbele ya Mwanakondoo.

Taarifa ya Jumla:

Neno "nikaona" inamzungumzia Yohana.

Mwanakondoo

Huyu ni mtoto wa kiume wa kondoo. Hapa hutumika kuashiria kuwa ni Kristo.

144,000

"laki moja na elfu arobaini na nne"

wenye jina lake na jina la Baba yake limeandikwa katika vipaji vya nyuso zao

"ambao kwenye vipaji vyao vya nyuso Mwanakondoo na Baba yake waliandika majina yao"

Baba yake

Hili ni jina muhimu la Mungu linaloeleza uhusiano kati ya Mungu na Yesu.

sauti kutoka mbinguni

"mlio kutoka mbinguni"

Revelation 14:3

Wakiimba wimbo mpya

"Wale watu 144,000 waliimba wimbo mpya." Hii inafafanua sauti aliyosikia Yohana. "Sauti hiyo ilikuwa ni wimbo mpya waliouimba"

wenye uhai wanne

"kiumbe hai" au "kitu chenye uhai"

wazee

Hii inamaanisha wazee ishirini na nne walikuwa wamekizunguka kiti cha enzi"

hawakujichafua wenyewe kwa wanawake

Maana zinazowezekana ni 1) "hawajawahi kuwa na mahusiano mabaya ya kimwili na mwanamke" au 2) "hawajawahi kukutana kimwili na mwanamke." Kujitia najisi na wanawake inaweza kuwa alama ya kuabudu sanamu.

maana walijitunza wenyewe dhidi ya matendo ya zinaa

Maana zinazowezekana ni 1) "hawakukutana na kimwili na mwanamke ambaye hakuwa mke wao" au 2) "ni mabikira."

walimfuata Mwanakondoo popote alipoenda

Kufanya kile afanyacho Mwanakondoo kinazungumziwa kama kumfuata. "wanafanya kile ambacho Mwanakondoo anafanya" au "wanamtii Mwanakondoo"

Hakuna uongo uliopatikana katika vinywa vyao

"kinywa" chao kinamaanisha kile walichosema. "Hawakuwahi kudanganya walipozungumza"

Revelation 14:6

Kauli Unganishi:

Yohana anaanza kuelezea sehemu ifuatayo ya maono yake. Huyu ni malaika wa kwanza kati ya watatu wanaotamkia dunia hukumu.

kila taifa, kabila, lugha, na watu

Hii humaanisha watu kutoka kila kabila.

Kwa maana muda wa hukumu yake umekaribia

Kuwepo katika wakati wa sasa unazungumziwa kama umekuja. Wazo la "hukumu" linaweza kuoneshwa na kitenzi. "sasa ni muda wa Mungu kuhukumu watu"

Revelation 14:8

Umeanguka, umeanguka Babeli mkuu

Malaika anaizungumzia Babeli kuangamizwa kama vile imeanguka. "Babeli kuu imeangamizwa"

Babebi kuu

"Babeli, ule mji mkuu" au "mji muhimu wa Babeli." Huu unawezekana kuwa ulikuwa ni alama ya mji wa Rumi ambao ulikuwa mkubwa, tajiri na wenye dhambi.

uliwanywesha

Babeli inazungumziwa kana kwamba ni mtu badala ya mji uliojaa watu.

kunywa divai ya tamaa zake mbaya

hii ni alama ya kushiriki katika tamaa zake mbaye za uasherati. "kuwa muasherati kama yeye" au "kulewa kama yeye na dhambi za uasherati"

tamaa mbaya

Babeli inazungumziwa kama vile ni kahaba aliyesababisha watu wengine watende dhambi pamoja naye. Hii inaweza kuwa na maana mara mbili: uasherati halisi na pia kuabudu miungu.

Revelation 14:9

kwa sauti kuu

"kwa sauti"

pia atakunywa divai ya ghadhabu ya Mungu

Kunywa divai ya ghadhabu ya Mungu ni alama ya kuadhibiwa na Mungu. "pia watakunywa sehemu ya divai inayowakilisha ghadhabu ya Mungu.

kumwagwa bila kuchanganywa

"kwamba Mungu amechanganya nguvu kamili"

kumwagwa bila kuchanganywa

Hii inamaanisha divai imechanganywa na divai zingine tu na wala hakuna maji yaliochanganywa humo. Ina nguvu, na mtu atakayeinywa nyingi atalewa sana. Kama alama, inaonesha kuwa Mungu atakuwa na hasira sana, sio hasira kidogo.

kikombe cha hasira yake

Mfano wa kikombe hiki kinashikilia divai inayowakilisha hasira ya Mungu.

malaika zake watakatifu

"malaika watakatifu wa Mungu"

Revelation 14:11

Kauli Unganishi:

Malaika wa tatu anendelea kuzungumza.

Na moshi wa maumivu yao

Maneno "maumivu yao" inamaanisha moto unaowatesa. "moshi kutoka katika moto unaowatesa"

hawakuwa na mapumziko

"hawana nafuu" au "mateso hayakomi"

mchana au usiku

Sehemu hizi mbili za siku zinatumika kumaanisha muda wote. "wakati wote"

Huu ni wito wa subira na uvumilivu kwa walio watakatifu

"Wale ambao ni watakatifu lazima wadumu kwa uvumilivu na kwa uaminifu"

Revelation 14:13

wafu wafao

"wale waliokufa"

wafao katika Bwana

"walioungana na Bwana na kufa." Hii inaweza kumaanisha watu waliouawa na adui zao. "walikufa kwa sababu wameungana na Bwana"

kazi

shida na mateso

matendo yao yatawafuata

Matendo haya yanazungumziwa kana kwamba yako hai na yanaweza kuwafuata waliyoyatenda. Maana zinazowezekana ni 1)"wengine watajua matendo mema waliyotenda watu hawa" au 2)"Mungu atawazawadia kwa matendo yao."

Revelation 14:14

Kauli Unganishi:

Yohana aanza kueleza sehemu inayofuata ya maono yake. Hii sehemu inahusu Mwana wa Adamu anapovuna dunia. Kuvuna nafaka ni ishara ya Mungu kuhukumu watu.

mfano wa Mwana wa Mtu

Huu usemi unafafanua umbo la binadamu, mtu anayefanana na binadamu.

taji ya dhahabu

Hii ilikuwa ni mfano wa shada la matawi ya mizeituni au majani ya laurusi yaliyopondwa kwenye dhahabu. Mifano yake iliyoundwa walipewa wanariadha washini kuvaa vichwani mwao.

mundu

kifaa kikali kama kisu au panga kilicho na mkunjo kwa ajili ya kukatia nyasi, nafaka na mizabibu.

kutoka kwenye hekal

"kutoka kwenye hekalu la kimbinguni"

muda wa mavuno umeshawadia

Kuwepo kwa wakati uliopo inazungumziwa kama umekuja.

dunia ikavunwa

"alivuna dunia"

Revelation 14:17

Kauli Unganishi:

Yohana anaendelea kuelezea maono yake ya dunia kuvunwa.

aliyekuwa na mamlaka juu ya moto

Hapa "mamlaka juu ya" inamaanisha jukumu la kuujali moto.

Revelation 14:19

pipa kubwa la divai ... Chujio la divai

Hii inamaanisha chombo kimoja.

pipa kubwa la divai ya ghadhabu ya Mungu

"pipa kubwa la divai ambapo Mungu ataonesha ghadhabu yake"

hatamu

kifaa kilochotengenezwa na ngozi che kuzungushwa kwenye kichwa cha farasi ili kumuongoza.

stadia 1,600

"kilomita 300" au "maili 200"

Revelation 15

Ufunuo 15 Maelezo kwa jumla

Muundo na mpangilio

Matukio na picha zinazofafanuliwa hapa inatokea mbinguni.

Tafsiri zingine zinaingiza ndani kidogo msitari wa ushairi ili isomeke kwa urahisi. ULB hufanya hivi na ushairi ulioko katika 15:3-4

Dhana muhimu katika sura hii

"Mahali patakatifu, ambamo kulikuwa na hema la mashahidi palifunguka mbinguni"

Maelezo haya yamefanya wasomi wengine kuamini kwamba hekalu la Wayahudi lilikuwa na mandhari ya mbinguni. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#heaven na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#writing-apocalypticwriting)

Nyimbo

Mbinguni mara nyingi huelezewa kama mahali ambapo watu wanaimba.Hizo ni nyimbo za ibada kwa Mungu. Hii inaashiria kwamba mbinguni ni mahali ambapo Mungu anaabudiwa kila mara.

<< | >>

Revelation 15:1

Taarifa ya Jumla:

Huu mstari ni ufupi wa kitakachotokea katika 15:6-16:21.

kubwa na yenye kushangaza

Maneno haya yanamaana za kukaribiana na yanatumika kwa msisitizo. "jambo lililo nishangaaza sana"

malaika saba wenye mapigo saba

"malaika saba waliokuwa na mamlaka ya kutuma mapigo saba duniani"

ambayo yalikuwa mapigo ya mwisho

"na baada yake, hayatakuwapo mapigo mengine tena"

katika hayo hasira ya Mungu ilikuwa imetimilika

"kwa kuwa mapigo haya yatakamilisha ghadhabu ya Mungu." maana zinazowezekana ni 1) mapigo haya yataonesha hasira yote ya Mungu au 2) baada ya mapigo haya, Mungu hatakuwa na hasira tena.

Revelation 15:2

Taarifa ya Jumla:

Hapa Yohana anaanza kueleza maono yake ya watu waliomshinda mnyama na wanamsifu Mungu.

bahari la bilauri

Inaainisha wazi jinsi ilivyokuwa kama kioo au bahari. Maana zinazowezekana ni 1) bahari linazungumziwa kama vile ni kioo. "bahari lililo laini kama kioo" au 2) kioo kinazungumziwa kama vile ni bahari. "kioo kilichosambazwa kama bahari"

wale waliokuwa washindi dhidi ya mnyama na sanamu yake

Jinsi walivyokuwa washindi inaweza kuelezwa vizuri. "wale waliokuwa washindi dhidi ya mnyama na sanamu yake kwa kutowaabudu."

juu ya namba inayowakilisha jina lake

Jinsi walivyokuwa washindi dhidi ya namba inaweza kuelezwa vizuri. "juu ya namba inayowakilisha jina lake na kwa kutowekwa alama ya namba hio"

namba inayowakilisha jina lake

Hii inamaanisha namba inayoelezwa katika 13:18.

Revelation 15:3

Walikuwa wakiimba

"Wale waliokuwa washindi dhidi ya mnyama walikuwa wakiimba"

Nani atashindwa kukuhofu wewe Bwana na kulitukuza jina lako?

Swali hili linatumika kuonesha kushangazwa kwao na jinsi gani Bwana alivyo mkuu na mtukufu. Inaweza kuelezwa kama mshangao. "Bwana, watu wote watakuogopa na kutukuza jina lako!"

kulitukuza jina lako

Usemi huu "jina lako" inamaanisha Mungu. "na kukutukuza wewe"

matendo yako yamejulikana

"umewafanya watu wote wajue matendo yako mema"

Revelation 15:5

Kauli Unganishi:

Malaika saba na mapigo saba wanatoka katika mahali patukufu zaidi. Zilizungumziwa katika 15:1.

Baada ya mambo hayo

"Baada ya watu kumaliza kuimba"

malaika saba wenye mapigo saba

Malaika hawa walionwa wakishilia mapigo saba kwa sababu walipewa mabakuli yaliojaa ghadhabu ya Mungu katika 15:7.

kitani

nguo ya gharama iliyotengenezwa kwa kitani.

mishipi

Mshipi ni kipande cha nguo cha urembo kinachovaliwa sehemu ya juu ya mwili.

Revelation 15:7

wenye uhai wanne

"viumbe wanne" au "vitu vinne vyenye uhai"

mabakuli saba ya dhahabu yaliyojaa ghadhabu ya Mungu

Picha ya divai katika bakuli inaweza kuelezwa vizuri. Neno "ghadhabu" hapa inamaanisha adhabu. Divai ni alama ya adhabu. "mabakuli saba yaliojaa divai inayoashiria ghadhabu ya Mungu"

mpaka mapigo saba ya malaika saba yalipokamilika

"mpaka malaika saba walipomaliza kutuma yale mapigo saba duniani"

Revelation 16

Ufunuo 16 Maelezo kwa jumla

Muundo na mpangilio

Sura hii ni hitimisho la sehemu kubwa ya kitabu cha Ufunuo ambayo inamalizia kipindi cha hasira ya Mungu ama hukumu kubwa inaletwa na Mungu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#judge)

Tafsiri zingine zinaingiza ndani kidogo msitari wa ushairi ili isomeke kwa urahisi. ULB hufanya hivi na ushairi ulioko katika 16:5-7

Dhana muhimu katika hii sura

"Mahali patakatifu sana"

Maelezo haya yamefanya wasomi wengine kuamini kwamba hekalu la Wayahudi lilikuwa na mandhari ya mbinguni. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#heaven na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#writing-apocalypticwriting)

Hukumu za mabakuli saba

Sura hii inafunua hukumu zinazoitwa hukumu za mabakuli saba. Hukumu hizi zimepewa taswira kama zile ambazo zinamwagwa inje kuashiria haraka na ujumla wa hizo hukumu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

Maswala mengine ya utata katika tafsiri ya sura hii

Hisia ya sura hii inakusudiwa kumshtua msomaji. Hii isipunguzwe kwenye tafsiri.

Har-Magedoni

Hili ni neno la Kiebrania na linatumika kama jina la mahali. Yohana anatafsiri herufi za neno hili kwa kuziandika kwa herufi za Kigriki. Watafsiri wanashauriwa kulitafsiri kutumia herufi za lugha kusudiwa.

<< | >>

Revelation 16:1

Kauli Unganishi:

Yohana aendelea kuelezea sehemu ya maono kuhusu malaika saba na mapigo saba. Mapigo saba ni mabakuli ya ghadhabu ya Mungu.

Nikasikia

Aliyesikia ni Yohana.

mabakuli ya ghadhabu ya Mungu

Picha ya divai katika bakuli inaweza kuelezwa vizuri. Neno "ghadhabu" hapa inamaanisha adhabu. Divai ni alama ya adhabu. "mabakuli saba yaliojaa divai inayoashiria ghadhabu ya Mungu"

Revelation 16:2

kumwaga bakuli lake

Neno "bakuli" linamaanisha kile kilichomo. "kumwagwa divai kutoka katika bakuli lake" au " kumwaga ghadhabu ya Mungu kutoka katika bakuli lake"

majeraha mabaya

"majeraha yenye maumivu." Haya yanaweza kuwa maambukizo kutoka kwa magonjwa au majeruhi ambayo hayajapona.

alama ya mnyama

Hii ilikuwa alama ya kuonesha kuwa aliyekuwa nayo alimwabudu mnyama.

Revelation 16:3

alimwaga bakuli lake

Neno "bakuli" linamaanisha kile kilichomo. "kumwagwa divai kutoka katika bakuli lake" au " kumwaga ghadhabu ya Mungu kutoka katika bakuli lake"

bahari

Hii inamaanisha maziwa yote ya maji ya chumvi na mabahari.

Revelation 16:4

akamwaga bakuli lake

Neno "bakuli" linamaanisha kile kilichomo. "kumwagwa divai kutoka katika bakuli lake" au " kumwaga ghadhabu ya Mungu kutoka katika bakuli lake"

mito na katika chemichemi za maji

Hii inamaanisha mikusanyiko yote ya maji safi.

malaika wa maji

Maana zinazowezekana ni 1) hii inamaanisha malaika wa tatu aliye juu ya kumwaga ghadhabu ya Mungu katika mito na chemichemi za maji au 2) huyu alikuwa ni malaika mwingine aliyekuwa juu ya maji yote.

Wewe ni mtakatifu

"Wewe" inamaanisha ni Mungu.

Wewe uliyepo na uliyekuwepo

"Mungu aliyepo na aliyekuwepo."

walimwaga damu za waamini na manabii

Hapa "walimwaga damu" inamaanisha kuuawa. "watu waovu waliwaua waamini na manabii"

umewapa wao kunywa damu

Mungu atawafanya watu waovu wanywe maji atakayoyabadili kuwa damu.

Nikasikia madhabahu ikijibu

Neno "madhabahu" hapa inamaanisha mtu madhabahuni. "Nikasikia mtu madhabahuni akijibu"

Revelation 16:8

akamwaga kutoka kwenye bakuli

Neno "bakuli" linamaanisha kile kilichomo. "kumwagwa divai kutoka katika bakuli lake" au " kumwaga ghadhabu ya Mungu kutoka katika bakuli lake"

likapewa ruhusa kuunguza watu

Yohana analizungumzia jua kama mtu. "na akasababisha jua kuwachoma watu kwa ukali"

Waliunguzwa kwa joto lenye kutisha

"Lile joto kali sana liliwachoma vibaya"

wakalikufuru jina la Mungu

Hapa jina la Mungu linamuwakilisha Mungu. "walimkufuru Mungu"

mwenye nguvu juu ya mapigo yote

Usemi huu unawakumbusha wasomaji kuhusu jambo ambalo wanalijua kumhusu Mungu. Linasaidia kueleza kwa nini watu walimkufuru Mungu. "kwa sababu ana nguvu juu ya mapigo yote haya"

guvu juu ya mapigo yote

Hii inamaanisha nguvu ya kusababisha haya mapigo kwa watu, na nguvu ya kuyasitisha mapigo.

Revelation 16:10

akamwaga kutoka kwenye bakuli lake

Neno "bakuli" linamaanisha kile kilichomo. "kumwagwa divai kutoka katika bakuli lake" au " kumwaga ghadhabu ya Mungu kutoka katika bakuli lake"

kiti cha enzi cha mnyama

Hapa ndipo mnyama anapotawalia. Inaweza kumaanisha mji mkuu wa ufalme wake.

giza likaufunika ufalme wake

Giza linazungumziwa kama vile ni kitu kama blangeti. "ikawa giza katika ufalme wake wote" au " ufalme wake wote ukawa giza"

Walisaga ... Wakamtukana

Hapa inamaanisha watu katika ufalme wa mnyama.

Revelation 16:12

limwaga kutoka kwenye bakuli lake

Neno "bakuli" linamaanisha kile kilichomo. "kumwagwa divai kutoka katika bakuli lake" au " kumwaga ghadhabu ya Mungu kutoka katika bakuli lake"

maji yake yakakauka

"Na maji yake yalikauka" au "Na kusababisha maji yake kukauka"

zilizoonekana kama chura

Chura ni mnyama mdogo anayeishi karibu na maji. Wayahudi waliwafikiria kuwa wanyama wachafu.

joka

Hili lilikuwa tambaazi kubwa kali, kama mjusi. Kwa wayahudi ilikuwa ni alama ya uovu na machafuko. Joka pia linatambulika katika mstari wa 9 kama "ibilisi au Shetani"

Revelation 16:15

Taarifa ya Jumla:

Mstari wa 15 ni mapumziko kutoka katika masimulizi makuu ya maono ya Yohana. Haya ni maneno yaliyonenwa na Yesu. Masimulizi yanaendelea mstari wa 16.

Tazama! Ninakuja

Inaweza kuwekwa wazi kwamba Bwana Yesu ndiye aliyesema haya katika UDB. Mabano yanatumika hapa kuonesha kuwa sio sehemu ya masimulizi ya maono.

Ninakuja kama mwizi!

Yesu atakuja wakati watu hawatarajii kama vile mwizi ajavyo asipotarajiwa.

atunzaye mavazi yake

Kuishi njia sahihi inazungumziwa kama mtu kutunza mavazi yake. "kufanya kilicho sahihi kama mtu atunzavyo mavazi yake mwilini"

atunzaye mavazi yake

Tafsiri zingine hutafsiri, "kukaa na mavazi yake"

kuiona aibu yake

Hapa "watakaoina" ni watu wengine.

Waliwaleta pamoja

"roho za mapepo ziliwaleta wafalme na majeshi yao pamoja"

sehemu iliyoitwa

"sehemu watu waitayo"

Amagedoni

Hili ni jina la sehemu.

Revelation 16:17

Kauli Unganishi:

Malaika wa saba amwaga bakuli la saba la ghadhabu ya Mungu.

alimwaga kutoka kwenye bakuli lake

Neno "bakuli" linamaanisha kile kilichomo. "kumwagwa divai kutoka katika bakuli lake" au " kumwaga ghadhabu ya Mungu kutoka katika bakuli lake"

Kisha sauti kuu ikasikika kutoka hekaluni na kutoka kwenye kiti cha enzi

Hii inamaanisha mtu aliyekuwa kwenye kiti cha enzi au karibu na kiti cha enzi alinena kwa sauti ku. Haiko wazi ni nani anayezungumza.

miale ya mwanga wa radi

Mwanga unaotokea wakati radi ikipiga.

ngurumo, vishindo vya radi

Hii ni miungurumo ya sauti ambayo radi husababisha.

Mji mkuu uligawanyika

"Tetemeko liliugawanya mji mkuu"

Kisha Mungu akakumbuka

"Kisha Mungu akawazia" au "Kisha Mungu akaanza kuwa makini na." Hii haimaanishi kuwa Mungu alikumbuka jambo alilosahau.

akaupa mji huo kikombe kilichokuwa kimejaa divai kutoka kwenye ghadhabu yake iliyo kali

Divai ni isharaya ya ghadhabu yake. Kuwafanya watu kuinywa ni ishara ya kuwaadhibu. "aliwafanya watu wa mji huo kunywa divai inayoashiria ghadhabu yake"

Revelation 16:20

Kauli Unganishi:

Hii ni sehemu ya bakuli la saba la ghadhabu ya Mungu.

milima haikuonekana tena

Kutokuweza kuiona milima ni mfano wa maneno yanayoeleza wazo ya kwamba milima haikuwepo tena. "milima haikuwepo tena"

talanta

"kilo 34"

Revelation 17

Ufunuo 17 Maelezo kwa jumla

Muundo na mpangilio

Sura hii ni uendelezo wa sura iliyopita.

Dhana muhimu katika sura hii

Kahaba

Wayahudi walionyeshwa mara nyingi kama watu wazinzi na wakati mwingine kama mkahaba. Hayo siyo maelezo yalioko hapa. Muktadha huu unamtambulisha shetani kama kahaba lakini mtafsiri ayafanye haya maelezo yasiwe wazi kabisa. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#writing-apocalypticwriting)

Vilima saba

Huenda hii inaashiria mji wa Roma uliosemekana kujengwa juu ya vilima saba. Hata hivyo, mtafsiri asijaribu kutambulisha hivi vilima saba katika tafsiri.

Tamathali muhimu za usemi katika sura hii

Mifano

Yohana anatumia mifano nyingi katika sura hii. Anapeyana maelezo fulani ya maana yazo lakini anaziacha kubaki kutoeleweka kwa kiwango fulani. Mtafsiri ajaribu kufanya namna hivyo. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

Maswala mengine ya utata katika tafsiri ya sura hii

"Na yule mnyama uliyemwona alikuwako, naye hayuko, naye yu tayari kuja "

Kauli hii imekusudiwa kutoa utofautisho na kauli ya kwamba Yesu "alikuwa na yuko na yu tayari kuja" ambayo imetumika kwingine kwenye maandiko (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-explicit)

Matumizi ya ukweli kinza

Ukweli kinza ni kauli ambayo inaonekana kujipinga ingawa siyo ya kipumbafu. Sentenzi katika 17:11 ni ukweli kinza"yule mnyama ...ni mfalme wa nane ingawa pia ni mmoja wa wale wafalme saba." Mtafsiri asijali kutatua ukweli huu kinza na ubakie kuwa siri. (Ufunuo 17:11)

<< | >>

Revelation 17:1

Taarifa ya Jumla:

Yohana anaanza kueleza sehemu ya maono yake kuhusu kahaba mkuu.

hukumu ya kahaba mkuu akaaye juu ya maji mengi

Nomino "hukumu" linaweza kuelezwa na kitenzi "kuhukumu". "jinsi gani Mungu atamhukumu kahaba mkuu aliyeketi juu ya maji mengi"

kahaba mkuu

"kahaba ambaye kila mmoja anamfahamu." Anawakilisha mji flani wenye uovu.

juu ya maji mengi

"juu ya mito mingi"

na juu ya mvinyo wa uasherati wake wakaao duniani wameleweshwa

Divai inawakilisha uasherati. "Watu wa duniani walilewa kwa kunywa divai yake, ambayo ni, walikuwa washerati"

uasherati wake

Hii inaweza kuwa na maana mbili: uasherati miongoni mwa watu na pia kuabudu miungu.

Revelation 17:3

akanichukua katika Roho mpaka nyikani

Mazingira yanabadilika kutoka kwa Yohana kuwa mbinguni na kuwa nyikani.

mawe ya thamani, na lulu

"aina nyingi za mawe ya dhamani"

lulu

Shanga nzuri na za dhamani. Zinaundwa ndani ya ganda la mnyama fulani mdogo aishiye baharini.

Juu ya paji la uso wake limeandikwa jina

"Mtu aliaandika jina kwenye paji la uso wake"

Babeli mkuu

Kama inahitajika kuwekwa wazi kwamba jina linamaanisha yule mwanamke, inaweza kuwekwa katika sentesi. "Mimi ni Babeli, yule mwenye nguvu"

Revelation 17:6

Taarifa ya Jumla:

Malaika anaanza kumueleza Yohana maana ya yule kahaba na mnyama mwekundu. Malaika anaeleza mambo haya hadi mstari wa 18.

alikuwa amelewa damu

"amelewa kwa sababu alikunywa damu"

waliokufa kwa ajili ya Yesu

"waumini waliokufa kwa sababu waliwaambia wengine kuhusu Yesu"

mshangao

"staajabu" au "shangazwa"

Kwa nini unashangaa?

Malaika alitumia swali hili kumkemea Yohana kwa upole. "Hautakiwi kushangaa!"

Revelation 17:8

shimo lisilo na mwisho

Hili ni shimo refu sana. Maana zinazowezekana ni 1)shimo halina mwisho chini; inaendelea kwenda chini zaidi milele au 2) shimo ni refu sana hata linakuwa kana kwamba halina mwisho.

Kisha ataendelea na uharibifu

Nomino "uharibifu" inaweza kutafsiriwa na kitenzi. "Kisha ataangamizwa" au "Kisha Mungu atamuangamiza"

ataendelea na uharibifu

Uhakika wa kile kitakachotokea baadae kinazungumziwa kana kwamba mnyama anaendako.

wale ambao majina yao hayakuandikwa

"wale ambao majina yao hayajaandikwa na Mungu"

tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu

"kabla Mungu hajaumba ulimwengu"

Revelation 17:9

Kauli Unganishi:

Malaika anaendelea kuzungumza. Hapa anafafanua maana ya vichwa saba vya mnyama ambavyo mwanamke amepanda.

Wito huu

"hii inaifanya ulazima kuwa"

Wito huu ni kwa ajili ya akili zilizo na hekima

Nomino "akili" na "hekima" zinaweza kuelezwa na "fikiri" na "kwa hekima." Kwa nini akili yenye hekima inahitaji inaweza kuwekwa wazi. "Akili yenye hekima inahitaji ili kuelewa hili" au "Unahitaji kufikiria kwa hekima ili kuelewa hili"

Vichwa saba ni milima saba

Hapa "ni" inamaanisha "kusimamia," "wakilisha."

Wafalme watano wameanguka

Malaika anazungumzia kufa kama kuanguka. "Wafalme watano wamekufa"

mmoja yupo

"mmoja ni mfalme sasa" au "mfalme mmoja yu hai sasa"

mwingine hajaja bado; wakati atakapokuja

Kutokuwepo inazungumziwa kama bado hajafika. "mwingine bado hajawa mfalme; akiwa mfalme"

atakaa kwa muda mfupi tu

Malaika anazungumzia kuhusu mtu kuendelea kuwa mfalme kana kwamba anabaki mahali fulani. "atakuwa mfalme kwa muda mfupi tu"

Revelation 17:11

ni mmoja wa wale wafalme saba

Maana zinazowezekana ni 1) mnyama anatawala mara mbili: kwanza kama mmoja wa wafalme saba, na kisha kama mfalme wa nane au 2) mnyama yuko katika kundi la hao wafalme saba kwa sababu ni kama wao.

anaenda kwenye uharibifu

Uhakika wa kile kitakachojiri mbeleni kinazungumziwa kana kwamba mnyama anaendako. "hakika itaangamizwa" au "Mungu hakika ataiangamiza"

Revelation 17:12

Kauli Unganishi:

Malaika anaendelea kuzungumza na Yohana. Hapa anaelezea maana ya mapembe kumi ya mnyama.

kwa saa moja

"kwa muda mfupi sana" au "kwa sehemu ndogo sana ya siku"

Hawa wana shauri moja

"Hawa wote wanawaza kitu kimoja" au "Hawa wote wanakubaliana kufanya kitu cha pamoja"

Mwanakondoo

Huyu ni mtoto wa kiume wa kondoo. Hapa hutumika kuashiria kuwa ni Kristo.

walioitwa, waliochaguliwa, na waaminifu

Hii inamaanisha kundi moja la watu. ""Walioitwa, kuchaguliwa , na waaminifu" au " wale ambao Mungu amewaita na kuwachagua na walio waaminifu kwake"

Revelation 17:15

Yale maji uliyoyaona, hapo alipoketi yule kahaba ni watu, makutano, mataifa na lugha

Hapa "ni" inamaanisha "yanawakilisha"

maji

"mito mingi"

makutano

"makundi makubwa ya watu" au "idadi kubwa ya watu"

lugha

Hii inamaanisha watu wanaozungumza hizo lugha.

Revelation 17:16

watamfanya kuwa mpweke na uchi

"kuiba kila kitu alichonacho na kumuacha bila kitu"

watamla mwili wake

Kumuangamiza kabisa inazungumziwa kama kula mwili wake. "watamuangamiza kikamilifu"

Maana Mungu ameweka mioyoni mwao kubeba kusudi lake kwa makubaliano ... yatakapotimia

Watakubali kumpa mnyama nguvu zao, lakini haitakuwa kwamba wanataka kumtii Mungu. "Kwa kuwa Mungu ataweka mioyoni mwao kukubali kumpa mnyama uwezo wao kutawala hadi maneno ya Mungu yatimie, na kwa kufanya hivi, watakamilisha mpango wa Mungu.

Mungu ameweka mioyoni mwao

Moyo unaashiria hamu. Kuwafanya kutaka kufanya kitu inazungumziwa kama kuweka mioyoni mwao. "Mungu amewafanya watake"

nguvu za kutawala

"mamlaka" au "mamlaka ya kifalme"

mpaka maneno ya Mungu yatakapotimia

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "mpaka Mungu atimize alichosema kitatokea"

Revelation 17:18

Kauli Unganishi:

Malaika amaliza kuzungumza na Yohana kuhusu kahaba na mnyama.

ni

Hapa "ni" inamaanisha "anawakilisha"

mji ule mkubwa utawalao

Inaposema mji unaotawala, inamaanisha kwamba kiongozi wa mji anatawala. "mji mkuu ambaye kiongozi wake anatawala"

Revelation 18

Ufunuo 18 Maelezo kwa jumla

Muundo na mpangilio

Sura ya 19 itaendeleza mambo yaliomo kwenye sura hii na sura zote zichukuliwe kama kipengele kimoja.

Tafsiri zingine zinaingiza ndani kidogo msitari wa ushairi ili isomeke kwa urahisi. ULB hufanya hivi na ushairi ulioko katika 19:1-8

Dhana muhimu katika sura hii

Unabii

Malaika anapeana unabii kuhusu kuanguka kwa Babeli. Inazungumziwa kana kwamba ishatokea ingawa haijatokea. Hii ilikuwa ni kawaida katika unabii na unasisitiza kutokuepuka kwa hukumu ijayo. Inatabiriwa pia watu wataomboleza kuanguka kwa Babeli. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#prophet, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#judge na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#writing-apocalypticwriting)

Tamathali muhimu sa usemi katika sura hii

Mifano

Mifano mara nyingi hutumiwa katika unabii. Sura hii inaachana kidogo na mfumo wa kiapokalipti wa kitabo hiki cha Ufunuo. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

<< | >>

Revelation 18:1

Kauli Unganishi:

Malaika mwingine ashuka toka mbinguni na kuzungumza. Huyu ni malaika tofauti na yule wa sura iliyopita, aliyezungumza kuhusu kahaba na mnyama.

Taarifa ya Jumla:

Anayezungumziwa hapa ni kama mtu ni mji wa Babeli.

Umeanguka, umeanguka, ule mji mkuu Babeli

Malaika anazungumzia Babeli kuangamizwa kama vile kuanguka.

ndege achukizaye

"ndege anayeudhi" au "ndege isyevutia"

mataifa yote

Mataifa ni njia nyingine ya kusema kwa watu wa mataifa hayo. "watu wa mataifa hayo"

yamekunywa mvinyo ya tamaa ya uovu wake

Hii ni ishara ya kushiriki katika tamaa zake za uasherati. "yamekuwa na uasherati kwama yeye" au "yamelewa na uasherati wake"

tamaa ya uovu wake

Babeli inazungumziwa kana kwamba ni kahaba aliyesababisha watu wengi wafanye dhambi pamoja naye. Hii inaweza kuwa na maana mara mbili: uasherati halisi na kuabudu miungu.

Wafanya biashara

Mfanya biashara ni mtu anayeuza vitu.

kwa nguvu ya maisha yake ya anasa

"kwa sababu alitumia pesa nyingi sana kwa ajili ya uasherati"

Revelation 18:4

Kauli Unganishi:

Sauti nyingine kutoka mbinguni inazungumza.

Taarifa ya Jumla:

Anayezungumziwa kama mtu ni mji wa Babeli, ambao unazungumziwa kama vile ni kahaba.

sauti nyingine

Neno "sauti" inamaanisha msemaji, ambaye huwezekana kuwa ni Yesu au Baba. "mtu mwingine"

Dhambi zake zimerundikana juu mpaka mbinguni

Sauti inazungumzia dhambi za Babeli kama vile ni vitu vinavyoweza kuunda rundo. "Dhambi zake ni nyingi sana ni kama rundo linalofika mbinguni"

ameyakumbuka

"akawazia" au "akaanza kuwa makini na." Hii haimaanishi kuwa Mungu alikumbuka jambo alilosahau.

Mlipeni kama alivyowalipa wengine

Sauti inazungumzia adhabu kana kwamba ni malipo. "Muadhibu kama alivyowaadhibu wengine"

mkamlipe mara mbili

Sauti inazungumzia adhabu kana kwamba ni malipo. "muadhibu mara mbili zaidi"

katika kikombe alichokichanganya, mchanganyishieni mara mbili kwa

Sauti inazungumzia kusababisha wengine kuteseka kama kuandaa divai yenye nguvu kwa ajili yao kunywa. "muandalie divai ya mateso ambayo ina nguvu mara mbili zaidi ya ile aliyowaandalia wengine" au "mfanyeni ateseke mara mbili zaidi ya alivyowatesa wengine"

mchanganyishieni mara mbili

Maana zinazowezekana ni 1)"andaa mara mbili ya kipimo" au 2)"ifanye kuwa na nguvu mara mbili zaidi"

Revelation 18:7

Kauli Unganishi:

Sauti ile ile kutoka mbinguni inaendelea kuzungumzia Babeli kana kwamba ni mwanamke.

alivyojitukuza

"watu wa Babeli walijitukuza"

Nimekaa kama malkia

Anadai kuwa mtawala, akiwa na mamlaka yake mwenyewe.

siyo mjane

Anadokeza kuwa hatakuwa tegemezi kwa watu wengine.

sitaona maombolezo

Kupitia maombolezo inatajwa kama kuona maombolezo. "sitawahi kuomboleza"

mapigo yake yatakuja

Kuwepo wakati wa mbeleni inazungumziwa kama yanakuja.

Atateketezwa kwa moto

Kuchomwa na moto inazungumziwa kama kuliwa na moto. "Moto utamchoma kikamilifu"

Revelation 18:9

Kauli Unganishi:

Yohana anasema kile watu wanachosema kuhusu Babeli.

Taarifa ya Jumla:

Hapa anayezungumziwa kama mtu ni mji wa Babeli.

waliofanya uasherati na kuchanganyikiwa pamoja naye

"kutenda dhambi za ngono na kufanya chochote walichotaka kama watu wa Babeli walivyofanya"

hofu ya maumivu makali

Maumivu makali yanaweza kutafsiriwa kama kitenzi. "wakihofu kuwa watateswa kama Babeli" au "wakihofu kuwa Mungu atawatesa kama anavyoitesa Babeli"

Ole, ole

Hii inarudiwa kwa ajili ya msisitizo.

adhabu yako imekuja

Kuwepo katika wakati wa sasa inazungumziwa kama ilimefika.

Revelation 18:11

kuomboleza kwa ajili yake

"kuomboleza kwa ajili ya watu wa Babeli"

mawe ya thamani, lulu

"aina nyingi za mawe ya dhamani"

kitani nzuri

nguo ya gharama iliyotengenezwa kwa kitani.

zambarau

"nguo ya zambarau"

hariri

Hii ni nguo laini, imara iliyotengenezwa kutoka kwenye nyuzi bora kama nondo wa hariri wanapotengeneza vifukofuko vyao. "nguo ya gharama" au "nguo bora" au "nguo nzuri"

nyekundu

"nguo nyekundu"

kila chombo cha pembe za ndovu

"kila aina ya chombo kilichoundwa na pembe za ndovu"

pembe za ndovu

Mali kigumu na kizuri cheupe ambacho watu wanaotoa kutoka kwenye pembe au meno ya wanyama wakubwa sana kama tembo na sili wa baharini. "mapembe" au "meno ya dhamani ya wanyama"

marumaru

jiwe la dhamani linatumika kwenye ujenzi.

mdalasini

kiungo cha mapishi chenye harufu nzuri na kinatoka katika gome la aina fulani ya mti.

kiungo

kitu kinachotumika kuongeza ladha kwenye chakula au harufu nzuri kwenye mafuta.

Revelation 18:14

Tunda

Wanazungumzia vitu vizuri kama vile ni tunda. "Vitu vizuri"

uliyoyatamani kwa nguvu zako zote

"ulitaka sana"

hayatapatikana tena

Kutokupatikana inamaanisha kutokuwepo. uu ni usemi. "hautayaona tena"

Revelation 18:15

Taarifa ya Jumla:

Katika mistari hii, anayezungumziwa kama binadamu ni mji wa Babeli.

kwa sababu ya hofu ya maumivu yake

Nomino "hofu" na "mateso" zinaweza kuelezwa na misemo inayoweza kuonesha ni nani aliyehisi hofu na maumivu makali. "kwa sababu watahofia jinsi atakavyoteswa"

wakilia na kuomboleza kwa sauti

Hiki ndicho watakachokifanya wafanya biashara. "na watalia na kuomboleza kwa sauti"

mji ule mkuu uliovikwa kitani nzuri

Katika sura hii yote, Babeli inazungumziwa kama vile ni mwanamke. Wafanya biashara wanaizungumzia Babeli kama vile imevaa kitani nzuri kwa sababu watu wake walikuwa wamevaa kitani nzuri. "ule mji mkuu, ulio kama mwanamke aliyevaa kitani nzuri" au "ule mji mkuu, ambao wanawake wake walivaa kitani nzuri"

uliovikwa kitani nzuri

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "uliovaa kitani nzuri"

na kupambwa kwa dhahabu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "na kujipamba mwenyewe kwa dhahabu" au "na kujipamba wenyewe kwa dhahabu" au "na kuvaa dhahabu"

vito vya thamani

"vito vinavyodhaminiwa"

lulu

Shanga nzuri na za dhamani. Zinaundwa ndani ya ganda la mnyama fulani mdogo aishiye baharini.

kipato chao kinatoka baharini

Msemo "kutoka baharini" inamaanisha kile wanachokifanya baharini. "wanaosafiri baharini kujikimu kimaisha" au "wanaosafiri baharini kwenda sehemu tofauti ili kufanya biashara ya vitu"

Revelation 18:18

Taarifa ya Jumla:

Katika mistari hii, neno "wa" inamaanisha mabaharia na wanamaji, na yule mtu mmoja anayezungumziwa ni ule mji wa Babeli.

Ni mji gani unafanana na mji huu mkubwa?

Swali hili linawaonesha watu umuhimu wa mji wa Babeli. "Hakuna mji mwingine kama mji ule mkuu, Babeli"

Mungu ameleta hukumu yenu juu yake

Nomino "hukumu" inaweza kuelezwa na kitenzi "kuhukumu." "Mungu amemuhukumu kwa ajili yenu" au "Mungu amemuhukumu kwa sababu ya maovu aliyowatendea"

Revelation 18:21

Kauli Unganishi:

Malaika mwingine aanza kuzungumzia Babeli. Huyu ni malaika tofauti na yule aliyezungumza awali.

jiwe kuu la kusagia

Jiwe kubwa la duara linatumika kusaga nafaka.

abeli, ule mji mkuu, utatupwa chini kwa nguvu na hautaonekana tena

Mungu atauangamiza ule mji kikamilifu. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mungu ataitupa Babeli kwa nguvu, ule mji mkuu, na haitakuwepo tena"

hautaonekana tena

"na hakuna mtu atakayeuona tena." Kutokuonekana hapa inamaanisha kwamba haitakuwepo tena. "haitakuwepo tena"

Sauti ya wapiga vinanda, wanamuziki, wacheza filimbi, na tarumbeta hawatasikika tena kwenu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Hakuna mtu katika mji wenu ambaye atasikia tena sauti ya wapiga vinanda, wanamziki, na wacheza filimbi, na sauti ya tarumbeta"

kwenu

Malaika anazungumza kana kwamba Babeli alikuwa hapo akimsikiliza. "ndani ya Babeli"

hawatasikika tena kwenu

"hakuna mtu atakayewasikia tena." Kutosikiwa hapa inamaana ya kutokuepo. "hawatakuwepo katika mji wenu tena"

Hakuna fundi ... hataonekana kwenu

Kutopatikana humo inamaana hawatakuwemo. "Hakuna fundi yeyote atakaye kuwa katika mji wenu"

Hakuna sauti ya kinu itakayosikika tena kwenu

Sauti ya kitu kutokusikika inamaana kwamba hakuna atakaye sikia hiyo sauti. "Hakuna atakaye tumia vinu katika mji wenu"

Revelation 18:23

Kauli Unganishi:

Malaika aliyetupa jiwe la kusagia anamaliza kuongea.

Taarifa ya Jumla:

Maneno "yako," "wako," na yake" inamaanisha ni Babeli.

Sauti ya bwana harusi na bibi harusi hazitasikiwa tena ndani yako

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Hakuna ambaye atasikia tena ndani ya Babeli sauti za furaha za bwana harusi na bibi harusi"

hazitasikiwa tena ndani yako

"hakuna atakaye visikia ndani yenu tena." Kutosikiwa hapa inamaanisha havitakuwepo" "havitakuwa ndani ya mji wenu tena"

wafanyabiashara wako walikuwa wakuu wa nchi

Malaika anazungumzia watu muhimu na wenye nguvu kama vile walikuwa wana wa wafalme. "wafanya biashara wenu walikuwa kama wana wa waflame duniani" au "wafanya biashara wenu walikuwa watu muhimu zaidi duniani"

mataifa, wamedanganywa kwa uchawi wako

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "uliwadanganya watu wa mataifa na uchawi wako"

Ndani yake damu ya manabii na waamini ilionekana, na damu ya wote waliouawa juu ya nchi

Damu kukutwa ndani yake ina maana kuwa watu walikuwa na hatia ya kuua watu. "Babeli inahatia ya kuua manabii na waumini na watu wengine wote waliouawa"

Revelation 19

Ufunuo 19 maelezo ya jumla

Muundo na mpangilio

Sura ya 19 inaendeleza maswala yalyomo katika sura ya 18 na kwa hivyo zote mbili zichukuliwe kama kipengele kimoja.

Tafsiri zingine zinaingiza ndani kidogo msitari wa ushairi ili isomeke kwa urahisi. ULB hufanya hivi na ushairi ulioko katika 19:1-8

Dhana muhimu katika sura hii

Nyimbo

Mbinguni mara nyingi huelezewa kama mahali ambapo watu wanaimba.Hizo ni nyimbo za kumwabudu Mungu. Hii inaashiria kwamba mbinguni ni mahali ambapo Mungu anaabudiwa kila mara. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#heaven)

Sherehe za harusi

Sherehe za harusi ama karamu ni ishara muhimu inayotumika katika maandiko.Katika utamaduni wa Wayahudi, paradiso ama maisha pamoja na Mungu baada ya kifo ilipewa taswira ya karamu. Hapa Yesu anaipatia taswira ya karamu ya harusi ambayo mfalme huandalia mwana wake wa kiume ambaye ameoa sasa hivi. Mbali na hiyo, Yesu anasisitiza kwamba siyo watu wote Mungu hualika watajiandaa vilivyo ili washiriki. Watu kama hawa watatupwa nje ya karamu.

<< | >>

Revelation 19:1

Taarifa ya Jumla:

Hii ni sehemu ya maono ya Yohana ifuatayo. Hapa anaelezea furaha ya mbinguni juu ya kuanguka kwa kahaba mkuu, ambaye ni mji wa Babeli.

nilisikia

Hapa aliyesikia ni Yohana.

Haleluya

Neno hili linamaana "Msifu Mungu" au "Tumsifu Mungu."

kahaba mkuu

Hapa Yohana anamaanisha mji wa Babeli ambao watu wake waouvu wanawatawala watu wote duniani na kuwaongoza kuabudu miungu ya uuongo. Anawazungumzia watu waovu wa Babeli kana kwamba ni kahaba mkuu.

aliyeiharibu nchi

Hapa "nchi" ni njia nyingine ya kusema wakazi. "waliwaharibu watu wa duniani"

damu ya watumishi wake

Hapa "damu" ni njia nyingine ya kuwakilisha mauaji. "kuwaua watumishi wake"

yeye mwenyewe

Hii inamaanisha Babeli. Kurudiwa kwa haya maneno ni kwa ajili ya kuongeza msisitizo.

Revelation 19:3

walisema

Hapa waliosema ni umati wa watu mbinguni.

Haleluya

Neno hili linamaana "Msifu Mungu" au "Tumsifu Mungu."

Moshi hutoka kwake

Huu udondoshaji wa maneno. Unaweze kujumuisha maneno yaliyokosekana ambayo yameonyeshwa bila kutajwa. "Moshi wa moto unaowaka katika mji utainuka"

hutoka kwake milele na milele

"kutoka kwa waabudu sanamu milele na milele" au "kwa wale walioshiriki kwenye ukahaba watateseka milele"

hutoka kwake

Hapa anayezungumziwa ni Babeli.

wazee ishirini na wanne

wazee wanne -"wazee 24"

viumbe hai wanne

"viumbe wanne wenye uhai" au "vitu vinne vyenye uhai"

akaaye kwenye kiti cha enzi

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "aliyeketi kwenye kiti cha enzi"

Revelation 19:5

sauti ilitoka kwenye kiti cha enzi

Hapa Yohana anazungumzia "sauti" kana kwamba ni mtu. "mtu alizungumza kutoka kwenye kiti cha enzi"

Msifuni Mungu wetu

Hapa "wetu" inamaanisha mnenaji na watumishi wote wa Mungu.

ninyi mnaomcha yeye

Hapa ina maana ya kumheshimu Mungu. "wote mnaomheshimu Mungu"

wote wasio na umuhimu na wenye nguvu

Mnenaji anatumia maneno haya pamoja kumaanisha watu wote wa Mungu.

Revelation 19:6

Ndipo nilisikia sauti kama sauti ya kundi kubwa la watu, kama sauti ya ngurumo ya maji mengi, na kama ngurumo ya radi

Yohana anazungumzia anachokisia kama vile ilikuwa sauti iliyotengenezwa na umati mkubwa sana wa watu, maji mengi wanayotiririka kwa kasi, na ngurumo ya radi kubwa.

Haleluya

Neno hili linamaana "Msifu Mungu" au "Tumsifu Mungu."

Bwana ni

"Kwa sababu Bwana"

Revelation 19:7

Kauli Unganishi:

sauti ya umati kutoka mstari uliopita yaendelea kuzungumza.

tushangilie

Hapa wanaoshangilia ni watumishi wa Mungu.

kumpa utukufu

"kumpa Mungu utukufu" au "kumheshimu Mungu"

harusi na sherehe ya Mwana Kondoo ... bibi harusi yuko tayari

Hapa Yohana anazungumzia kuunganishwa pamoja kwa Yesu na watu wake kwama vile sherehe ya harusi.

Mwanakondoo

Huyu ni mtoto wa kiume wa kondoo. Hapa hutumika kuashiria kuwa ni Kristo.

imekuja

Kuwepo katika wakati wa sasa inazungumziwa kama imekuja.

bibi harusi yuko tayari

Yohana anawazungumzia watu wa Mungu kana kwamba ni bibi harusi anayejianda kwa ajili ya harusi yake.

Aliruhusiwa kuvalishwa kitani safi na yenye kung'aa

Hapa aliyevaa ni watu wa Mungu. Yohana anazungumzia matendo ya haki ya watu wa Mungu kana kwamba ni nguo safi za kung'aa ambazo bibi harusi huvaa siku ya harusi yake. Unaweza kueleza hii kwa hali ya kutenda. "Mungu alimruhusu kuvaa nguo kitani ya safi na ya kung'aa.

Revelation 19:9

Taarifa ya Jumla:

Malaika anaanza kuzungumza na Yohana. Hii inawezekana kuwa malaika yule yule aliyeanza kuzungumza na Yohana katika 17:1.

walioalikwa

Unaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "watu ambao Mungu amewakaribisha"

sherehe ya harusi ya Mwana kondoo

Hapa malaika anazungumzia kuunganishwa kwa Yesu na watu wake kama vile ni sherehe ya harusi.

Nilisujudu

Kusujudu ni kula chini kwenye ardhi, uso ukitazama chini, kuonesha heshima na utayari wa kutumika.

ndugu zako

Neno "ndugu" hapa inamaanisha waumini wote wa kiume na wa kike.

wenye kuushika ushuhuda wa Yesu

Hapakushika inamaansiha kuamini au kutangaza. "wanaosema ukweli kuhusu Yesu"

kwa kuwa ushuhuda wa Yesu ni roho ya unabii

Hapa "roho ya unabii" inamaanisha Roho Mtakatifu wa Mungu. "kwa sababu ni Roho wa Mungu anayewapa watu nguvu ya kunena ukweli kuhusu Yesu"

Revelation 19:11

Taarifa ya Jumla:

Hapa ni mwanzo wa maono mengine. Yohana anaanza kuelezea mpandaji wa farasi nyeupe.

Kisha niliona mbingu zimefunguka

Hii picha inatumika kuashiria mwanzo wa maono mapya.

yule aliyekuwa amempanda

Aliyempanda ni Yesu.

Huhukumu kwa haki

Hapa "haki" inamaanisha kile kilicho sahihi. "Anahukumu watu wote kulingana na kile kilicho sahihi"

Macho yake ni kama mwali wa moto

Yohana anazungumzia macho ya mpandaji kama vile yaling'aa kama mwali wa moto.

jina lililoandikwa juu yake

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mtu ameandika jina juu yake"

asilolifahamu mtu yeyote isipokuwa yeye mwenyewe

"Yeye tu ndiye ajuae maana ya jina hilo"

Amevaa vazi lililochovywa katika damu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Damu imefunika vazi lake"

jina lake anaitwa Neno la Mungu

Unaweza kueleza hii kwa hali ya kutenda. "jina lake pia ni Neno la Mungu"

Revelation 19:14

Kinywani mwake hutoka upanga mkali

Ubapa wa upanga ulikuaunchomoza kinywani mwake. Upanga wenyewe haukua ukisogea.

huyaangamiza mataifa

"huyapiga mataifa" au "anayamudu mataifa"

atawatawala kwa fimbo ya chuma

Yohana anazungumzia nguvu ya mpandaji kama vile anatawala na fimbo ya chuma.

Naye hukanyaga vyombo vya mvinyo kwa hasira kali ya Mungu

Yohana anazungumzia mpandaji kuangamiza adui zake kana kwamba ni zabibu ambazo mtu anakanyaga kwenye chombo cha mvinyo. Hapa "hasira" inamaanisha adhabu ya Mungu kwa watu waovu. "Atawakanyaga adui zake kulingana na hukumu ya Mungu, kama tu binadamu anavyokanyaga zabibu kwenye chombo cha mvinyo"

Naye ameandikwa juu ya vazi lake na katika paja lake jina

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mtu ameandika jina kwenye vazi lake na kwenye paji:"

Revelation 19:17

Niliona malaika amesimama katika jua

Hapa "jua" ni njia nyingine ya kusema mwanga wa jua. "Kisha nikaona malaika akisimama kwenye mwanga wa jua"

walio huru na watumwa, wasio na umuhimu na wenye nguvu

Malaika anatumia makundi mawili ya maneno yenye tofauti pamoja kumaanisha watu wote.

Revelation 19:19

Mnyama alikamatwa na nabii wake wa uongo

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mpandaji wa farasi nyeupe alimkamata mnyama na nabii wa uongo"

chapa ya mnyama

Hii ilikuwa alama ya kuonesha kuwa aliyekuwa nayo alimwabudu mnyama.

Wote wawili walitupwa wangali hai

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mungu alimtupa mnyama na nabii wa uongo wangali hai"

katika ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti

"ziwa la moto liwakalo salfa" au "sehemu ilyojaa moto unaowaka salfa"

Revelation 19:21

Wale waliobaki waliuawa kwa upanga uliotoka kinywani mwa mmoja aliyepanda juu ya farasi

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mpandaji wa farasi aliwaua wanajeshi waliosalia wa mnyama kwa upanga uliotoka kinywani mwake"

uliotoka kinywani mwake

Ubapa wa upanga ulikuaunchomoza kinywani mwake. Upanga wenyewe haukua ukisogea.

Revelation 20

Ufunuo 20 Maelezo ya jumla

Muundo na mpangilio

Sura hii inahusu kipindi kinachojulikana kama "ufalme wa kimilenia" kwa sababu ni ufalme wa miaka elfu moja. Sura hii ni muhimu kuelewa matukio ya siku za mwisho na kitabu cha Ufunuo.(Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#lastday)

Dhana muhimu katika sura hii

Miaka elfu ya utawala wa Kristo

Yesu anaelezewa kama anayetawala kwa miaka elfu moja na nabii zote za maandiko kuhusu amani duniani kote lazima zitatimika. Wasomi wanatofautiana kuhusu iwapo huu ni muda wa ekweli ama ni ishara ya mwanzo wa utawala wa Kristo kwenye mioyo ya watu. Ni vizuri kutafsiri kana kwamba Kristo anatawala kimwili duniani kwa miaka elfu moja na siyo kujaribu kuweka taswira ya kimafumbo katika maandiko. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#prophet)

Uasi wa mwisho

Sura hii inafafanua kipindi cha wakati baada ya utawala wa Yesu kinachojulikana kama uasi wa mwisho.Wakati huu,Shetani na watu wengi watajaribu kuasi dhidi ya Yesu. Hii itapelekea ushindi wa mwisho wa Mungu dhidi ya dhambi na uovu kabla ya maisha ya milele kuanza. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#sin, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#evil na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#eternity)

Kiti kikubwa cheupe cha enzi

Hii ni hukumu muhimu mbinguni baada ya uasi wa mwisho.Wakati wa hukumu hii, watu walio na imani kwa Mungu wanatenganishwa na wale wanaomkataa. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#judge, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#heaven and https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#faith)

Tamathali muhimu za usemi katika sura hii

Kitabu cha uzima

Hii ni mfano wa maisha ya milele. Walio na uzima wa milele wanasemekana kuwa na majina yao yameandikwa katika kitabu hiki cha uzima.. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

Maswala mengine ya utata katika tafsiri ya sura hii.

Kuzimu na ziwa la moto

Hizi zinaoenakana kuwa mahali mbili tofauti. Mtafsiri anaweza kufanya utafiti zaidi kupata jinsi ya kuzitofautisha hizi mahali mbili lakini zisifananishwe katika tafsiri. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#hell)

<< | >>

Revelation 20:1

Taarifa ya Jumla:

Yohana anaanza kueleza maono ya malaika akimtupa ibilisi kwenye shimo lisilo na mwisho.

Kisha niliona

Hapa aliyeona ni Yohana.

shimo lisilo na mwisho

Hili ni shimo refu sana na jembamba. Maana zinazowezekana ni 1)shimo halina mwisho chini; inaendelea kwenda chini zaidi milele au 2) shimo ni refu sana hata linakuwa kana kwamba halina mwisho.

joka

alikuwa mtambaazi mkubwa na mkali, anayefanana na mjusi. Kwa wayahudi, hii ilikuwa ni alama ya uovu na mabaya.

kulitia mhuri juu yake

Malaika alilifunga shimo na kulitia muhuri ili mtu yeyote asifungue. "aliifunga na kuitia muhuri ili mtu yeyote asifungue"

asiwadanganye mataifa

Hapa "mataifa" ni njia nyingine ya kusema watu wa duniani. "asiwadanganye makundi ya watu"

miaka elfu

"miaka 1,000"

ataachiwa huru

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mungu atamuamuru malaika amuweke huru"

Revelation 20:4

Taarifa ya Jumla:

Hii ni sehemu ifuatayo ya maono ya Yohana. Anaelezea kuona ghafla viti vya enzi na roho za waumini.

walikuwa wamepewa mamlaka ya kuhukumu

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "wale ambao Mungu aliwapa uwezo wa kuhukumu"

ambao walikuwa wamekatwa vichwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "wale ambao vichwa vyao vilikatwa"

kwa ajili ya ushuhuda kuhusu Yesu

"kwa sababu walizungumza ukweli kuhusu Yesu"

Walikuja uzimani

"walifufuka" au "walikuwa hai tena"

Revelation 20:5

Wafu waliobaki

"watu wote wengine waliokufa"

miaka elfu ilipokuwa imeisha

"mwisho wa miaka 1,000"

Mauti ya pili haina nguvu juu ya watu hawa

Hapa Yohana anafafanua "mauti" kama mtu mwenye nguvu. "Watu hawa hawatapitia kifo cha pili"

Mauti ya pili

"kufa mara ya pili." Hii inaelezwa kama adhabu ya milele katika ziwa la moto la 20:13 na 21:7. "kifo cha mwisho ni ziwa la moto."

Revelation 20:7

Shetani atafunguliwa kutoka gerezani mwake

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mungu atamuachia Shetani kutoka katika gereza lake"

kona nne za dunia

Hii ni lugha inayomaanisha "duniani kote"

Gogu na Magogu

Haya ni majina ambayo nabii Hezekia alitumia kuwakilisha mataifa ya mbali.

Watakuwa wengi kama mchanga wa bahari

Huu ni msisitizo wa namba kubwa sana la askari wa jeshi la Shetani.

Revelation 20:9

Walikwenda

"Jeshi la Shetani lilikwenda"

mji upendwao

Hii inamaanisha Yerusalemu.

moto ulikuja kutoka mbinguni na kuwaangamiza

Hapa Yohana anazungumzia moto kana kwamba ukko hai. "Mungu alituma moto toka mbinguni kuwachoma"

Ibilisi, ambaye aliwadanganya, alitupwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mungu alimtupa Ibilisi aliyewadanganya" au "Malaika wa Mungu walimtupa Ibilisi aliyewadanganya,"

ziwa liwakalo kiberiti

"ziwa la moto liwakalo kiberiti" au "sehemu ilyojaa moto unaowaka kiberiti"

ambamo mnyama na nabii wa uongo walikuwa wameshatupwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ambamo alikuwa amemtupa mnyama na nabii wa uongo"

Watateswa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mungu atawatesa"

Revelation 20:11

Taarifa ya Jumla:

Hii ni sehemu ifuatayo ya maono ya Yohana. Anaelezea kuona ghafla kiti cheupe cha enzi na wafu wakihukumiwa.

Dunia na mbingu zilikimbia mbali kutoka katika uwepo wake, lakini hapakuwako nafasi ya wao kwenda

Yohana anaelezea mbingu na nchi kama vile ni watu wanaojaribu kutoroka hukumu ya Mungu. Hii inamaanisha kuwa Mungu aliaangamiza kabisa mbingu na nchi za zamani.

hodari na wasio wa muhimu

Yohana anaunganisha maneno haya yenye maana tofauti kumaanisha watu wote waliokufa.

vitabu vilifunuliwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "mtu alivifunua vitabu"

Wafu walihukumiwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mungu aliwahukumu watu waliokuwa wamekufa na sasa wako hai tena"

kwa kile kilichoandikwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "kwa kile alichoandika"

Revelation 20:13

Bahari iliwatoa wafu ... Kifo na kuzimu viliwatoa wafu

Hapa Yohana anazungumzia bahari, kifo na kuzimu kana kwamba ni watu hai.

wafu walihukumiwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mungu aliwahukumu wafu"

Kifo na kuzimu zilitupwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mungu alizitupa kifo na kuzimu" au "Malaika wa Mungu walizitupa kifo na kuzimu"

kuzimu

Hapa "kuzimu" ni njia nyingine ya kusema mahali ambapo wasioamini wanapokwenda pale wanapokufa ili kusubiri hukumu ya Mungu.

mauti ya pili

"kufa mara ya pili." Hii inaelezwa kama adhabu ya milele katika ziwa la moto katika 20:13 na 21:7. "kifo cha mwisho ni ziwa la moto"

Kama jina la yeyote halikupatikana limeandikwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Kama malaika wa Mungu hawakupata jina la mtu"

litupwa ndani ya ziwa la moto

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "malaika alimtupa katika ziwa la moto" au "malaika alimtupa mahali ambapo moto unawaka milele"

Revelation 21

Ufunuo 21 Maelezo ya jumla

Muundo na mpangilio

Sura hii inatoa maelezo ya kina kuhusu Yerusalemu mpya.

Dhana muhimu katika sura hii

Kifo cha pili

Kifo ni aina ya muachano. Kifo cha kwanza ni kifo cha mwili, kuachana kwa roho kutoka kwa mwili. Kifo cha pili ni utengano wa milele kutoka kwa Mungu. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/other.html#death, https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#soul na https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#eternity)

Tamathali muhimu za usemi katika sura hii

Kitabu cha uzima

Hii ni mfano wa maisha ya milele. Wale walio na uzima wa milele husemekana kuandikwa majina yao wkenye kitabo hiki cha uzima. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tm/translate.html#figs-metaphor)

Maswala mengine ya utata katika tafsiri ya sura hii

Mbingu mpaya na dunia mpya

Haieleweki iwapo hii ni dunia na mbingu tofauti kabisa ama kama zitatengenezwa kutoka kwa dunia na mbingu za kisasa. Hii ni hali sawa na Yerusalemu mpya. Kuna uwezekano kwamba hii itaathiri tafsiri katika lugha zingine.

<< | >>

Revelation 21:1

Taarifa ya Jumla:

Yohana anaanza kueleza maono yake ya Yerusalemu mpya.

nikaona

Aliyeona ni Yohana.

kama bibi harusi aliyepambwa kwa ajili ya mumewe

Hii inaifananisha Yerusalemu mpya kama bibi harusi anayejipamba kwa ajili ya bwana harusi wake.

Revelation 21:3

Nilisikia sauti kubwa kutoka kwenye kiti cha enzi ikisema

Neno "sauti" inamaanisha yule anayezungumza. "mtu akinena kwa sauti kutoka katika kiti cha enzi akisema"

Tazama!

Nenno "Tazama" inatuweka macho kuwa makini na taarifa za kushangaza zifuatazo.

Makao ya Mungu yapo pamoja na wanadamu, naye ataishi pamoja nao

Misemo hii miwili inamaanisha kitu kimoja na inasisitiza kuwa, hakika, Mungu ataishi miongoni mwa watu.

Atafuta kila chozi kutoka katika macho yao

Machozi hapa yanawakilisha huzuni. "Mungu atafuta huzuni yao kama vile anafuta machozi yao" au "Mungu atawasababisha wasiwe na huzuni tena"

Revelation 21:5

maneno haya ni ya hakika na kweli

Hapa "maneno" yanamaanisha ujumbe uliyounda. "ujumbe huu ni wakuaminika na wa kweli"

Alfa na Omega, mwanzo na mwisho

Misemo hii miwili inamaanisha jambo moja na inasisitiza asili ya milele ya Mungu .

Alfa na Omega

Hizi ni herufi za kwanza na mwisho katika alfabeti ya Kigriki. Maana zinazowezekana ni 1) "yule aliyeanzisha vitu vyote na anayevileta mwisho vitu vyote" au 2)"yule ambaye alikuwepo na ataendelea kuwepo". Kama haieleweki kwa wasomaji unaweza kufikiria kutumia herufi katika alfabeti zako. "Yeye ni A na Z" au "mwanzo na mwisho"

mwanzo na mwisho

Maana zinazowezekana ni 1)"yule aliyeanzisha vitu vyote na ambaye atasababisha vyote kufika mwisho" (UDB) au 2) "yule aliyekuwepo kabla ya vitu vyote na atakuwepo baada ya vitu vyote."

Kwa yeyote aonaye kiu ... maji ya uzima

Mungu anazungumzia hamu ya uzima wa mile kama vile ni kiu na mtu anayepokea uzima wa milele ni kama vile anakunywa maji yaletayo uzima.

Revelation 21:7

Kauli Unganishi:

Aliyeketi katika kiti cha enzi aendelea kuzungumza na Yohana.

waoga

"wale wanaoogopa sana kufanya kilicho sahihi"

wachukizao

"wanaofanya vitu vibaya"

ziwa la moto wa kiberiti uunguzao

"ziwa la moto liwakalo kiberiti" au "sehemu ilyojaa moto unaowaka kiberiti"

mauti ya pili

"kufa mara ya pili." Hii inaelezwa kama adhabu wa milele katika ziwa lamoto katika 20:13 na 21:7. "kifo cha mwisho katika ziwa la moto."

Revelation 21:9

bibi harusi, mke wa mwana kondoo

Malaika anazungumzia Yerusalemu mpya kama vile ni mwanamke anayetaka kuolewa na bwana harusi wake, Mwanakondoo. Yerusalemu ni jina jingine la waumini watakao ushimo.

Mwanakondoo

Huyu ni mtoto wa kiume wa kondoo. Hapa hutumika kuashiria kuwa ni Kristo.

alinichukua mbali katika Roho

Mazingira yanabadilika na Yohana anapelekwa kwa mlima mrefu ambapo anaweza kuuona mji wa Yerusalemu.

Revelation 21:11

Yerusalemu

Hii inamaanisha "Yerusalemu kushuka kutoka mbinguni" ambayo ameieleza katika mstari uliopita na sio Yerusalemu halisia.

kama kito cha thamani, kama jiwe la yaspi jeupe kama kioo

yaspi safi - Misemo hii miwili inamaanisha kitu kimoja. Ya pili inasisitiza ubora wa Yerusalemu kwa kutaja bayana aina ya yaspi.

jeupe kama kioo

nyeupe* "nyeupe sana"

yaspi

Hili ni jiwe la dhamani. Yaspi inawezakana kuwa ilkuwa nyeupe kama kioo.

milango kumi na miwili

"milango 12"

pameandikwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "mtu aliapaandika"

Revelation 21:14

Mwanakondoo

Hii inamaanisha Yesu.

Revelation 21:16

stadia

Kiwanja cha michezo kinaurefu wa mita 185.

dhiraa

dhiraa ni sentimita 46.

Revelation 21:18

Ukuta ulikuwa umejengwa kwa yaspi na mji kwa dhahabu safi

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mtu aliujenga ukuta kwa yaspi na mji kwa dhahabu safi"

dhahabu safi, kama kioo safi

Dhahabu ilikuwa safi sana hadi inazungumziwa kama vile ilikuwa kioo.

Misingi ya ukuta ilikuwa imepambwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Mtu aliipamba misingi ya ukuta"

yaspi ... zumaridi ... akiki

Haya ni mawe ya dhamani. Yaspi inawezekana ilkuwa nyeupe kama kioo, na akii inawezekana ilikuwa nyekundu. Zumaridi ni kijani.

yakuti samawi ...kalkedon ... sardoniki ... krisopraso ... hiakintho ...amethisto

Hivi vyote ni vito vya dhamani.

Revelation 21:21

lulu

Shanga nzuri na za dhamani. Zinaundwa ndani ya ganda la mnyama fulani mdogo aishiye baharini.

kila mlango ulitengenezwa kutoka kwenye lulu moja

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "mtu alitengeneza kila mlango kutoka kwenye lulu moja"

hahabu safi, ikionekana kama kioo safi

Dhahabu ilikuwa safi sana hadi inazungumziwa kama vile ilikuwa kioo.

Bwana Mungu ... na Mwana Kondoo ni hekalu lake

Hekalu liliwakilisha uwepo wa Mungu. Hii inamaanisha Yerusalemu mpya haitahitaji hekalu kwa sababu Mungu na Mwanakondoo watakuwepo humo.

Revelation 21:23

taa yake ni Mwanakondoo

Hapa utukufu wa Yesu , Mwanakondoo, unazungumziwa kama vile ni taa inayotoa nuru kwa ajili ya mji.

Milango yake haitafungwa

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Hakuna atakayefunga milango yake"

Revelation 21:26

Wataleta

"Wafalme wa duniani wataleta"

hakuna kichafu kitakachoingia ndani yake kamwe

maneno hasi haya mawili yanaweza kusemwa kwa hali chanya kwa kusema "kile kilicho kisafi tu ndio kitaingia."

bali ni wale tu ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwanakondoo

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "lakini wale tu ambao Mwanakondoo ameandika majina yao katika kitabu cha Uzima"

Mwanakondoo

Huyu ni mtoto wa kiume wa kondoo. Hapa hutumika kuashiria kuwa ni Kristo.

Revelation 22

Ufunuo 22 Maelezo ya jumla

Muundo na mpangilio

Sura hii inasisitiza kwamba nabii za kitabu cha Ufunuo zinaenda kutimilika hivi karibuni. (Tazama: https://read.bibletranslationtools.org/u/WA-Catalog/sw_tw/kt.html#prophet)

Dhana muhimu katika sura hii

Mti wa uzima

Kuna uwezekano kwamba kulinuiwa kulinganisha mti wa uzima katika Bustani ya Edeni na mti wa uzima unaotajwa hapa. Laana ilioanza Edeni itaisha wakati huu.

Maswala mengine ya utata katika tafsiri ya sura hii

Alfa na Omega

Haya ni majina ya herufi za kwanza na za mwisho katika alfabeti ya Kigriki. ULB inafafanua majina yao kwa Kiingereza. Mpangilio huu unweza kuwa kielelezo cha watafsiri wengine. Watafsiri wengine, hata hivyo, wanaweza kuamua kutumia herufi za kwanza na za mwisho katika alfabeti zao, kwa mfano "A na Z " katika Kiingereza.

__<< | __

Revelation 22:1

Kauli Unganishi:

Yohana anaendelea kuelezea Yerusalemu mpya kadri malaika anavyomuonesha.

akanionesha

Hapa anayeoneshwa ni Yohana.

mto wa maji ya uzima

"mto unaotiririka maji yaletayo uzima"

maji ya uzima

Uzima wa milele unazungumziwa kana kwamba ni kinywaji cha maji yaletayo uzima.

Mwanakondoo

Huyu ni mtoto wa kiume wa kondoo. Hapa hutumika kuashiria kuwa ni Kristo.

mataifa

Hapa "mataifa" yanamaanisha watu wanaoishi katika kila taifa. "watu wa mataifa yote"

Revelation 22:3

Wala hapatakuwa na laana yoyote tena

Maana zinazowezekana ni 1) "Hakutakuwa na yeyote humo ... amabye Mungu atamlaani" (UDB) au 2) "Hakutakuwa na yeyote humo aliye chini ya laana ya Mungu."

watumishi wake watamtumikia

Maana zinazowezekana za "wake" ni 1) neno hili linamaanisha Mungu Baba, au 2) linamaanisha Mungu na Mwanakondoo ambao wote wanatawala pamoja kama mtu mmoja.

Revelation 22:6

Taarifa ya Jumla:

Huu ni mwanzo wa mwisho wa maono ya Yohana. Katika mstari wa 6 malaika anazungumza na Yohana. Katika mstari wa 7, Yesu anazungumza, kama ilivyoainishwa katika UDB.

maneno haya ni ya hakika na kweli

Hapa "maneno" yanamaanisha ujumbe uliyounda. "ujumbe huu ni wa kuaminika na wa kweli"

Mungu wa roho za manabii

Maana zinazowezekana ni 1) neno "roho" inamaanisha tabia ya ndani ya manabii na inaashiria kuwa Mungu ndio aliwapa msukumo. "Mungu aliyewaongoza manabii" (UDB) au 2) neno "roho" inamaanisha Roho Mtakatifu amabye aliwaongoza manabii. "Mungu aliyewapa manabii Roho wake"

Tazama!

Hapa Yesu anaanza kuzungumza. Neno "Tazama" inaongeza msistizo kwa kile kinachofuata.

Ninakuja upesi!

Inaeleweka kuwa anakuja ili kuhukumu. "Ninakuja kuhukumu upesi!

Revelation 22:8

Taarifa ya Jumla:

Yohana anawaambia wasomaji wake jinsi alivyomjibu malaika.

kulala kifudifudi

Hii inamaanisha kulala chini na kujinyoosha kwa sababu ya heshima na unyenyekevu. Hii nafasi ilikuwa sehemu muhimu katika kuabudu, kuonesha heshima na utayari wa kutumika.

Revelation 22:10

Kauli Unganishi:

Malaika anamaliza kuzungumza na Yohana.

Usiyatie muhuri ... kitabu hiki

Kutia muhuri kitabu ilikuwa kukifunga na kitu ambacho kilikifanya isiwezekane kwa yeyote kusoma kilichomo ndani hadi ule muhuri uvunjwe. Malaika alikuwa akimwambia Yohana kutoufanya ujmbe kuwa siri. "Usifanye siri ... kitabu hiki"

aneno ya unabii wa kitabu hiki

Hapa "maneno" yanamaanisha ujumbe uliyounda. "Huu ujumbe wa kinabii wa kitabu hiki"

Revelation 22:12

Taarifa ya Jumla:

Kitabu cha Ufunuo kikiwa kinafika mwisho, Yesu anatoa salamu zake za kufunga.

Alfa na Omega, wa Kwanza na wa Mwisho, Mwanzo na Mwisho

Misemo hii mitatu inafanana maana na inasisitiza kuwa Yesu alikuwepo na ataendelea kuwepo muda wote.

Alfa na Omega

Hizi ni herufi za kwanza na mwisho katika alfabeti ya Kigriki. Maana zinazowezekana ni 1) "yule aliyeanzisha vitu vyote na anayevileta mwisho vitu vyote" au 2)"yule ambaye alikuwepo na ataendelea kuwepo". Kama haieleweki kwa wasomaji unaweza kufikiria kutumia herufi katika alfabeti zako. "Yeye ni A na Z" au "mwanzo na mwisho"

wa Kwanza na wa Mwisho

Hii inamaanisha uasili wa Yesu wa milele.

Mwanzo na Mwisho

Maana zinazowezekana ni 1)"yule aliyeanzisha vitu vyote na ambaye atasababisha vyote kufika mwisho" (UDB) au 2) "yule aliyekuwepo kabla ya vitu vyote na atakuwepo baada ya vitu vyote."

Revelation 22:14

Kauli Unganishi:

Yesu anaendelea kutoa salamu zake za kufunga.

wale waoshao mavazi yao

Kuwa mtakatifu inazungumziwa kama mtu kuosha nguo zake. "wale waliokuwa watakatifu, kana kwamba wameosha mavazi yao"

Nje

Hii inamaanisha wako nje ya mji na hawaruhusiwi kuingia.

kuna mbwa

Kwenye utamaduni huo, mbwa alikua ni mnyama mchafu anayechukiwa. Hapa neno ni lakumshusha mtu hadhi na linamaanisha watu waovu.

Revelation 22:16

kuwashuhudia

Hapa wanaoshuhudiwa ni wengi.

mzizi wa uzao wa Daudi

Maneno "mzizi" na "uzao" yanamaanisha kitu kimoja tu. Yesu anazungumzia kuwa "mzawa" kana kwamba ni "mzizi" uliota toka kwa Daudi. Kwa pamoja maneno haya yanasisitiza kuwa Yesu anatoka katika familia ya Daudi.

Nyota ya Asubuhi ing'aayo

Yesu anajizungumzia mwenyewe kuwa kama nyota inayoonekana asubuhi kabla ya kupambazuka na inaashiria kuwa siku mpya imekaribia kuanza.

Revelation 22:17

Kauli Unganishi:

Hili ni jibu kwa kile alichosema Yesu.

Bibi harusi

Waumini wanazungumziwa kana kwamba ni bibi harusi anasubiri kuolewa na bwana harusi, Yesu.

Njoo!

Maana zinazowezekana ni 1) kwamba huu ni ukaribisho wa watu kuja na kunywa maji ya uzima. "Njoni mnywe!" au 2) kwamba hili ni ombi la unyenyekevu la kumuomba Yesu arudi. "Tafadhali njoo!"

Yeyote aliye na kiu ... maji ya uzima

Hamu ya mtu kwa ajili ya uzima wa milele inazungumziwa kana kwamba ni kiu na kwa mtu huyo kupokea uzima wa milele kama vile kunywa maji yaletayo uhai.

maji ya uzima

Maisha ya milele yanazungumziwa kama vile ni kinywaji kiletacho uhai.

Revelation 22:18

Taarifa ya Jumla:

Yohana anatoa maneno yake ya mwisho juu ya kitabu cha Ufunuo.

Namshuhudia

Anayeshuhudia ni Yohana.

maneno ya unabii wa kitabu hiki

Hapa "maneno" yanamaanisha ujumbe yaliyounda. "Ujumbe huu wa kinabii wa kitabu hiki."

Kama yeyote ataongeza katika hayo ... Kama mtu yeyote atayaondoa

Hili ni onyo kali la kutobadili chochote kwenye utabiri huu.

yaliyoandikwa katika kitabu hiki

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ambayo nimeyaandika ndani ya kitabu hiki"

Revelation 22:20

Taarifa ya Jumla:

Katika mistari hii, Yohana anatoa salamu zake za kufunga pamoja na za Yesu.

Yeye ashuhudiaye

"Yesu, ashuhudiaye"

kila mtu

"kila mmoja wenu"